Search This Blog

Wednesday, November 18, 2020

X SEHEMU YA 9/10

   


X  

WRITER…………………………………………EDDAZARIA G.MSULWA


WEBSITE………………………………………… www.storyzaeddytz.com
CONTACT……………………………………….. 0657072588/0768516188
AGE……………..18+

SEHEMU YA 9 KATI YA 10


“Muheshimiwa raisi kuna tatizo”

Kauli ya Luteni Jenerali ikanifanya kukaa kitako kitandani.

“Tatizo gani?”

“Caro amajaribu kujiua kwa kujing’ata ulimiw ake hivyo madaktari wana jaribu kuyaokoa maisha yake na kwa sasa yupo chumba cha upasuaji”

“Ohoo Mungu wangu sasa kwa nini amefanya maamuzi hayo?”

“Hatujui kuna siri gani unayo ndelea kumtafuna hadi ameamua kujiua.”

“Sasa nisikilzie Luteni jenerali”

“Ndio muheshimiwa raisi”

“Nahitaji, mipaka, anga, bahari kute ulinzi uwe mara mbili na sasa. Nahitaji jeshi kuwa tayari kwa vita muda wowote. Nahitaji Satelaite zote ziwe macho kuhakikisha tuna jua kila kinacho endelea, tuna elewana?”

“Ndo muhehsimiwa raisi nimekuelewa”

“Nashukuru”

Nikakata simu huku Cauther akinitazama kwa macho ya udadisi.

“Kuna nini?”

“Caro amejing’ata ulimi wake akihitaji kujiua.”

“Ehee kwa nini sasa?”

“Sijui nahisi makossa yake yangemuhukumu vibaya”

“Umeona, laiti kama ungemuachia huru, angejiua, asinge kuwa na uwezo wa kuidhuru nchi.”

Mlango wa chumbani kwetu ukagogwa. Cauther akajifunga tenge na akatembea hadi mlangoni akaufungua.

“Dada muambie she mana wageni wake”

“Kutoka wapi?”

“Wamesema ni wazee wa chama”

Nilisikia mazungumzo hayo kati ya Cauther na Nadia.

“Wapo wapi?”

“Wapo sebleni ya wageni”

“Sawa waambia ana kuja”

“Haya”

“Mtoto ana sumbua?”

“Wala wajina wangu hasumbui nacheka cheka naye tu hapa”

“Sawa”

Cauther akafunga mlango.

“Sasa hao wamekuja kufanya nini?”

“Sijui mume wangu ita kuwa jambo jema kwenda kuwasikiliza”

“Njoo tuoge”

Mimi na Cauther kwa pamoja tukaoga, Cauther akaniandalia ngoa za kuvaa.

“Ila mume wangu wewe……”

Cauther alizungumza huku akitabasamu.

“Nini tena?”

“Yaani ni mtu wa tofauti sana. Sasa uliwezaje kutoroka kwenye hayo mashambulizi?”

“Yaani wee acha tu mke wangu. Haikuwa kazi rahisi, sema muda mwengine ni Mungu tu ana kuwa upande wangu ila kama si vinginevyo, ningefia Isreal”

“Nilikuombea mume wangu, nahisi pia Mungu alisikia maombi yetu”

“Ni kweli”

“Alafu siku nyingi hatujaenda Kanisani. Hembu jumapili hii twnede mume wangu tukatoe hata sadaya ya shukrani kwa maana umepunyuka kufa kufa huko. Mungu katupa mrembo mzuri tena kwenye kipindi ambacho ilisalia kidogo nipoteza maisha kwa ajili ya mstuko”

“Sawa mke wnagu uta pangilia ratiba ya kwenda kanisani na uta mjulisha mchungaji”

“Hakuna shaka mume wangu”

Tukatoka ndani hapa na mimi nikaelekea katika seble ambayo nina kutania na wageni wana kuja hapa ikulu na seble hii ni tofauti na seble ya nyumba ninayo ishi na familia yangu. Nikawakuta wazee wa chama nane ambao mmoja ni mwenyekiti, makamu mwenyekiti. Katibu mkuu wa chama na wajumbe wengine wa ngazi za juu. Nikawasalimia kwa heshima zaote.

“Karibuni sna wazee wangu”

“Tuna shukuru sana muheshimiwa raisi. Tumesikia tatizo lililo tokea hivyo tukaona sio mbaya kuja kujukulia hali kabla hata siku haijaisha na pia tusamehe kwa kuja bila ya taarifa”

“Ohoo musijali wazee wangu na tumesha poa, japo tumepoteza vijana mahiri, shupavu na wenye nguvu ya kulitumikia taifa hili. Ila walifanya kila liwezekanalo ili maisha yangu yabaki kuwa salama hadi sasa”

“Ni kweli ni jambo la heri. Muhshimiwa raisi sisi tumekuja na ajenda moja ama mbili ambazo tuna imani kwa usikivu wako na unyenyekevu wako uta tusikiliza”

“Hakuna shaka……Ahhaa samahani mara moja”

Niliwaomba msamaha wazee hawa kwani simu yangu ina ita na ni simu muhimu kutoka kwa lutein jenerali.

“Ndio”

“Muhshimiwa raisi Caro amefariki dunia saa moja na dakika kumi na mbili usiku huu, madaktari wamejiatahidi kufanya kila wanacho weza ila wameshindwa kuyaokoa maisha yake”

Nikajikuta nikishusha pumzi nyingi sana huku nikiwatazama wazee hawa ambao macho yao yote yapo kwangu. Kwani mtu niliye mpendekeza agombanie uraisi katika chaama chao ndio huyo amefariki dunia kwa kujiua.



“Sawa Luteni jenerali nimeipokea taarifa”

“Nashukuru mkuu”

Nikakata simu na kuiwekea pembeni ya sofa hili niliko kaa.

“Ndio wazee wangu”

“Muheshimiwa raisi tumekuja kukupa pole kwa yaliyo tokea na pia tumekuja na ombia moja ambalo kama nilivyo tangulia kusema. Wewe ni mtu mwenye hekima, mstarabu na mpole hivyo tungeomba sana kwenye hili utufikirie”

Mwenyekiti wa chama alizungumza huku akinitazama usoni mwanagu..

“Tuna tambua kwamba katiba ya nchi hairuhusu kwa wewe kugombania uraisi kutokana na umri wako kuwa bado mdogo. Ila tumependekeza ni kwa nini tusipitishe kura ya wananchi ambao ata kubali kwa uchaguzi huu umri wa mgombea uraisi ushushwe ili wewe ugombanie bila ya kikwazo chochote?”

“Na isitoshe muheshimiwa raisi una kubalika sana na watu huko mitaani. Yaani tuna uhakika tukikusimamisha wewe uta pita kwa asilimia mia moja”

“Jana ilipaswa niwe marehemu kutokana nahii kazi. Ila Mungu pekee ndio aliye nipa nafasi ya kuwa hapa japo myuma nimepoteza vijana wengie waio na hatia. Vijana ambao hawakupaswa kufa wakiwa katika majukumu kama haya.”

Nilizungumza kwa upole huku nikiendelea kuwatazama wazee hawa.

“Hii nchi yenye nguvu sana duniani. Kwa miaka kadhaa ya nyuma nchi yenye nguvu ilikuwa ni Marekani ambao kwa sasa ni wapili baada ya sisi kupanda na kuwa wa kwanza. Jambo musilo lijua ni kwamba mimi nina maadui wengi kuliko maraisi wote walio wahi kuiongoza hii nchi. Piga picha hadi walinzi wako binafsi wana hitaji kukuu au wamelipwa ili wakuue, una hisi nini hapo?”

Wazee hawa wakatazamana huku wakiwa katika nyuso za mshangao.

“Maana yake ni kwamba adui yako yupo sebleni mwangu. Nikifanya kosa ata nimaliza”

“U..una maanisha nini mkuu?”

“Simaanishi kwamba nyingi ndio maadui zangu. Hapana, adui mkubwa ni yule aliye nitengeneza mimi kuwa hivi”

“Nani huyo mkuu?”

“Mambo mengine ni mambo ya siri na vita yangu sinto hitaji kuliingiza taifa, lije kupoteza kiongozi mwengine au raisi wasio na hatia kisa mimi. Niacheni niende nikaendelee na maisha mengine. Kama ita tokea nikawa raisi basi ita kuwa ni kwa mapenzi ya Mungu ila kwa sasa tusijaribu kulazimisha mambo ambayo badae ina weza kutokea nikapoteza hekima, burasa ambayo muna iona sasa hivi na nikawa kama nduli Iddi Amin na nikawaua raia wangu mimi mwenyewe. Nina imani kwamba hii siku mutaijutia sana na kujiuliza ni kwa nini mulinishawishi na kuwa raisi wa hii nchi”

Nilizungumza kwa sauti ya upole sana na kuwafanya wazee hawa kushusha pumzi zao.

“Kutokana Caro amehusika kwenye mpango wa kunia. Kuna mtu nitapendekeza mumuangalie kwani yeye amefanya kazi na maraisi wawili, yule aliye uwawa na mimi. Mzee huyu ni mshauri wa wangu, ana uwezo mkubwa na maono makuba na ana jua siri nyingi za kiti cha uraisi. Pia umri wake una ruhusu sana kuwa kiongozi wa hii nchi”

“Ila ni mzee sana tuna hisi miaka yake ina fika sabibi na?”

“Ndio ni mzee. Ila uongozi una tokea hapa kichwani na sio kwenye umri. Kwani aliye ifanya hii nchi iwe ni nchi ya ajabu ni nani?”

Wazee hawa wakatazamana na wakakosa jibu la kunipa.

“Makamu wa raisi aliye pita. Yeye ndio anaye endesha genge moja kubwa sana la uhalifu duniani lina itwa Scorpion. Wao ndio wana maamuzi nani awe raisi na nani asiwe raisi yeye ndio mtu ambaye alinitengeneza mimi. Alinitoa kuwa kibaka mtaani hadi kuwa mtu hatari kwenye jeshi na tishio kwenye nchi. Muna jua ni kwa nini mimi na yeye ni maaduia?”

“Hapana mkuu”

“Kwa sababu aliwaua wezangu wasio na hatia. Tulitengenezwa kuwa silaha ya serikali, nina imani mulisikia kikosi cha X. Kilikuwa ni kikiso cha watu hatari, tulifanya mission ngumu na hatari na tulifaulu. Tulizunguka dunia kwa ajili ya kuikoa dunia. Tulihakikisha kwamba magaidi wa duia ninzima wana ipata joto ya jiwe. Muna jua nini kilicho tokea?”

“Hapana mkuu”

“Tulifanyiwa ambush na ambush hiyo ilipangwa na makamu wa raisi akishirikiana na hawa Scorpion. Hakuna mjanja mbele ya ambush na mbaya tulikuwa tuna pita njia za siri ambazo tuna imani hakuna mtu ambaye alikuwa ana fahamu kwamba tuna pita. Tulipigwa risasi nyingi sana. Tulijaribu kupambana ila tulishindwa mapambano kwa mara ya kwanza. Nilishushudia damu za ndugu zangu zikimwagika mbele ya macho yangu na roho zao zikitoka. Niliokoka kwenye vita hiyo na kuamua kuachana na jeshi hadi juzi juzi ndege ya raisi ilivyo tekwa ndivyo nami nikarudi kwenye kushika silaha.”

Nilizungumza kwa hisia kali huku machozi yakinilenga lenga na kuwafanya wazee hawa kukaa kimya huku wakinitazama kwa masikitiko.

“Juzi kuamkia jana tulifanyiwa ambushi tena na ilipangwa na makamu wa raisi pamoja na yule mwanamke niliye mpa umakamu wa raisi wa muda, kuna kipi nimebakisha kama sio kuuwawa. Nina mke, nina binti mchanga ambaye hata mwezi hana. Ningekufa jana ni historia gani angeipata kwa baba yake. Angejivunia nini kwa baba yake? Je ni historia ambayo angeadithiwa na mama yake au kuisoma kwenye vitabu ehee?”

Nilizungumza sasa kwa msisitizo huku machozi yakinimwagika kw achungu.

“Roho yangu ina windwa na siwezi kuwa kiongozi kwa sasa. Nahitaji kupata nafasi ya kwenda kupumzika mimi na make wangu ambaye toka nimemuoa, hatujawahi kukaa mwenzi mzima bila ya mimi kupata majukumu ya kikazi ambayo mwanzoni nilisha aapia kuachana nayo.”

Baada ya kuzungumza maneno hayo nikasimama.

“Tafuteni mtu wa kuwa raisi au kama muta chukua ushauri wangu wa kumfwata mshauri wamgu basi mfwateni ila kwa mimi musitegemee wala mukajipa matumaini ya kwamba niyta kuwa raisi. Asanteni na usiku mwema”

Nikaondoka sebleni hapa na kuwaacha wazee hawa wakiwa na maswali yaliyo kosa majibu. Nikarudi nyumbani kwagu.

“Vipi mume wangu mbona macho mekundu hivyo?”

“Nilikuwa nina waeleza ukweli wazee wa chama kwamba sina mpango wa kuwa raisi wa hii nchi”

“Kwa nini shem, ikiwa maisha ya ikulu hapa ni matamu sana”

Nadia alizungumza huku akinitazama.

“Matamu kwa wageni ambao wana kuja na kuliona hili jengo kwa nje na uzuri pamoja na mazingira yake ya ndani. Ila ni magumu sana kwa mtu anaye kuwa ana ongoza hii sheemu na nchi kwa ujumla. Hivyo shem kila jambo ni gumu”

“Mmmm”

“Ndio alafu kuna habari ya msiba mke wangu”

“Wa nani tena?”

“Caro amefariki”

“Weeee?”

“Yaa amefariki”

“Kwa hiyo walishindwa kuunga ulimi wake?”

“Silaha ya mwisho kwa jasusi yoyote anaye kamatwa na kutakiwa kutoa siri za kikosi chake ua nchi yake basi kama akishindwa kujiua kwa kutumia kidonge cha sumu basi ni kujing’ata ulima hadi kuwa vipande viwili na baada ya hapo maisha yake yanakuwa yanafika ikingoni”

“Weeee shem hivi kuna mtu ana weza kung’ata ulimi hadi ukakatika?”

“Ndio”

“Mmm si ina uma sana kwa maana mtu ukijing’ta kidogo tu una hisi kufa kufa?”

“Ndio hivyo shem”

“ila amevuna alicho kipanda”

Cauher alizungumza.

“Yaa hicho ndio alicho kivuna”

“Ila mume wangu ina bidi upate muda wa kupumzika. Nimesha pika chakula nina kuomba ukisha kula ukalale. Najua juzi hukulala na hadi una fika hapa nyumbani huja lala pia. Hivyo nakuomba ukalale”

“Asante mke wangu, leo umepika nini?”

“Nimepika chakula ukipendacho”

“Nini?”

“Nyama ya kuchoma na viazi vya kuchoma”

“Waoo”

“Yaa nimekutengenezea na kachumbani pamoja na juisi ya tende unayo ipenda”

“Una nikumbusha kipindi hicho nipo Beirut na wanajeshi wezangu. Tulikuwa tuna penda sana kula hivyo vitu”

“Kweli?”

“Yaa ndio chakula cha haraka haraka ambacho hakihitaji maandalizi mengi.”

Kwa pamoja tukapata chakula cha usiku na baada ya chakula hichi nikaingia chumbani kwangu na kulala fofofo.

“Honey, honey”

Niliisikia sauti ya Cauther kwa mbali.

“Mmmm”

“Mlinzi wako yupo mlangoni hapo ana kuita”

“Saa ngapi sasa?”

“Saa nane usiku”

“Ruben”

“Ndio mkuu”

Nikashuka kitandnai huku nikipiga miyayo ya uchovu mwingi nilio nao. Nikamtazama Cauther aliye jilaza pembeni yangu.

“Usumbufu huu”

“Pole mume wangu kamsikilize”

Nikashuka kitandani huku nikivaa suruali pamoja na shati, nikatoka chumbani hapa na kumkuta Ruben akiwa amesimama mlangoni.

“Muheshimiwa raisi kuna tatizo. Una hitajika commanding room”

“Tatizo gani?”

“Anga letu limevamiwa na ndege za jeshi la Israel na zimesha ingia kwenye zone yetu na tumejaribu kuwakanya wasiendelee kuingia kwenye anga letu ila wamekaidi agizo”

Nikavaa shati langu kwa haraka.

“Hujavaa kitu miguuni mkuu”

Nikaingia chumbani na kuvaa kobazi.

“Mke wangu nina kuja”

“Sawa”

Tukaanza kutembea kwenye kordo hii ndefu kuelekea katika chumba maalumu cha kuendeshea oparesheni za kiusalama. Watu wote wakasimama na nikatembea hadi kwenye screen kubwa iliyopo ndani hapa na kutazama ndege hizi aina ya jet nne zikiwa angani huku ndege zetu za jeshi nyingine nne zikiwa angani.

“Muhehsimiwa raisi”

Kijana mmoja akanikabidhi kinasa sauti na nikakivaa sikioni mwangu kwani kina niwezesha kuzungumza moja kwa moja na marubani wa ndege zetu za kijeshi.

“Wana semeje?”

Nilimuuliza mkuu wa jeshi la anga aliyopo katika makao makuu ya anga ambaye nina muona kwenye tv kubwa iliyopo pembeni.

“Tumejaribu kuwakanya mara kadhaa na kuwaeleza wana ingia kwenye anga la nchi ya Tanzania ila bado zina zidi kuisogelea Dar es Salaam”

“Muheshimiwa raisi ina bidi tuzishambulie”

“Wapeni onyo la kwanza”

Nilizungumza na yakachiwa makombora kama manne yaliyo piga mbele ya ndege hizi na marubani wa ndege hizo wakayakwepa kuonyesha kwamba hawahitaji kutii amri.

“Mkuu wana zidi kusogelea Dar es Salaam”

Rubani mmoja wa ndege alizungumza.

“Mkuu tuwashambulie”

Washauri wangu wa maswala ya usalmaa walizungumza huku wakinitazama usoni.

“Musiwashambulie nahitaji Jet nyingine nne ziwe juu ya anga la Dar es Salaam. Wasilianeni na raisi wa Israel”

“Ila muheshimiwa raisi kwa yote aliyo tufanyia una hitaji tuwasiliane naye”

“Wasilianeni naye”

“Sawa mkuu”

Simu ikapigwa Isarel na nikakabidhiwa nizungumze naye.

“Muheshimiwa raisi naona ndege zako zimeingia kwenye anga la nchi yangu. Unaweza kuniambia zina lengo gani kuingia nchini mwangu?”

“Wewe una isi zina lengo gani?”

“Una nijibu zina lengo gani kuingia kwenye anga langu. Nina imani una shuhuldiki kinacho endelea. Cheza na mimi nikiwa nje ya nchi yangu ila sio ndani ya nchi yangu kwani nilikula kiaapo kuilinda na kuitetea nchi yangu yangu”

Nikakata simu kisha nikatazama ndege hizi za jeshi zikiendelea kuwa angani.

“Nina waruhusu kuzishambulia”

“Sawa muheshimiwa raisi”

“Mapambano ya anga yakaanza ndege za jeshi la Tanzania hazikuwa na mchezo hata kidogo. Japo marubani wa ndege hizi wana jitahidi kujibu mashambulizi ila haikuwa rahisi kwama wanavyo dhani kwani ndege zetu zina uwezo wa hali ya juu na marubani wetu wamefunzwa kwa mafunzo ya hali ya juu. Ndani ya dakika kumi na tano ndege zote za jeshi la Israel zikaangushwa.

“Hongera san muheshimiwa raisi”

Washauri wangu alizungumza.

“Huu ni mtego ni lazima tuwe makini kwenye hili. Nahiji makombora ya nyuklia yawe tayari kwa kuishambulia Israel na musubirie amri yangu”

“Muheshimiwa una hitaji kuanzisha vita?”

“Wameanzisha vita. Nilikaa kimya na kusamehe kwa kilicho tokea Isarel leo wamenifwata hadi nyumbani nini munahitaji nifanye kama raisi. Munahitaji tuwasujudie kwa kuwa wao ni taifa teule la Mungu kwamba kila atakaye pigana nao ata angamizwa. So hii ni Tanzania nasi tumeteuliwa na Mungu, ni wapole na tuna amani, hatumchokozi mtu na atakaye tuchokoza tuna mpiga na Mungu ata kuwa upande wetu kwani hadi kufika hapa haikuwa bahati mbaya ila alikuwa na makusudi yake kutufikisha hapa. Tuna elewana?”

“Ndio muheshimiwa raisi”

Watu wote waliitikia.

“Ni kombora ngapi za nyuklia zina weza kuifuta Israel kwenye ramani ya dunia?”

“Si chini ya kombora ishirini nane, tutaipiga pande zote kumi na sita za dunia na tuta wasambaratisha”

“Sawa”

Mshauri wangu mkuu naye akaingia ndani hapa kwani alikuwa nyumbani kwake. Akanong’oenzana na baadhi ya washauri wezake kisha akanifwata sehemu nilipo simama.

“Mkuu na sikia una hitaji kuwashambulia wa Israel”

“Kama walivyo tushambulia nasi tuna rudisha mashambulizi”

“Ila muheshimiwa raisi kumbuka sio wote walio wabaya. Tusiasdhibu nchi nzima ikiwa kuna watu walio tusaidia kama kina Camel. Tafadhali muheshimiwa raisi tusichukue maamuzi hayo. Maamuzi haya yana fanywa na viongozi wachache wapuuz. Tafadhali muheshimiwa raisi nina kuomba hekima yako kwenye hilo”

Nikashusha pumzi nyingi huku nikimtazama mshauri wangu.

“Tafadhali”

Nikawatazama watu wote waliomo ndani hapa kwani wote wana sikiliza amri yangu.

“Una weza kuwasiliana na Camel”

“Ndio”

“Naomba umpigie sasa hivi kwa simu ya hapa”

“Sawa mkuu”

Simu ikapigwa na baada ya muda ikapokelewa.

“Ni mimi”

“Nashukuru Mungu mpenzi wangu upo salama”

“Raisi ana hitaji kuzungumza na wewe”

“Raisi Eddy?”

“Ndio”

“Muunganishe”

“Ndio madame”

“Muheshimiwa raisi nafuraha kusikia sauti yako”

“Nashukuru hata mimi mama yangu. Nina tatizo nina omba unisaidie’

“Zungumza tu kijana wangu”

“Raisi wako ameamrisha ndege za kijeshi kuvamia katika anga la nchi yangu”

“Mungu wangu”

“Na tumefanikiwa kuziangusha ndege hizo. Nina imani ana mpango mwengine wa kufanya dhidi ya nchi yangu hivyo nia kuomba jambo moja”

“Jambo gani?”

“Naomba umpindue kutoka madarakani, nita kupa msaada wa kila utakacho kihitaji ila nina kuomba ufanye mapinduzi ya nchi tadadhali.”

Ombi langu alikamfanya madame Camel kukaa kimya kwa sekunde kadha kwani swala la kupindua nchi sio jambo la mzaha mzaha na kama ata julikana basi ana weza kuuwawa kama msaliti wa nchi.



“Mmmm muheshimiwa raisi hilo ni wazo zuri na gumu pia kutekelezeka kama unavyo fahamu nchi yangu ni nchi ambayo ulinzi wa raisi ni muhimu kuliko kitu chochote hivyo ina bidi kuchukua muda sana katika kuliamua hilo”

“Najua madame ila kama una hitaji kupata vijana watakao kusaidia kwenye hilo”

“Sawa muheshimiwa raisi, ila ningependa tukutane na tuweze kukuzungumza kwa kina nisije nikawa kama Caro. Hahahaaa”

“Nashukuru na nina kukaribisha muda wowote kuja nchini Tanzania”

“Basi kesho majira ya saa tisa utarajie ugeni wangu kwako”

“Nashukuru sana

Nikakata simu huku nikimtazama mshauri wangu huyu.

“Kwa mfano akikata tuna fanyaje?”

Nilimuuliza mshauri wangu huku nikimtazama usoni mwake.

“Kama amekubali kuja hato weza kukataa”

“Una muamini?”

“Ndio muheshimiwa”

“Sawa ila huyu bwege kabla ya kupinduliwa nita hitaji kumuona kwa macho yangu namna anavyo kufa”

“Usijali mkuu uta muona tu”

“Alafu nimekumbuka. J ana wazee wa chama walinifwata kuniomba niweze kugombania katika chama chao ila nikakata na nikawapendekeza wakutafute wewe kwa maana umefanya kazi kwenye hii serikali, una ijua kuliko mtu yoyote yule anavyo ijua. Je wamekufwata?”

“Hapana hawajanifwata na pia umri wangu umekwenda sana Eddy nikiwa raisi wa hii nchi na hizi ngija ngija za kila siku naweza kufa kabla ya muda wangu. Hivyo sidhani kama nina weza kugombani uraisi. Ni mara tattu nimepunyuka kuuwawa ni kiwa na maraisi, wewe na aliye pita na mimi pekee ndio nimepata ujasiri wa kurudi ofisini huku wezangu wakiendelea na mapumziko. Nahitaji kupumzika mkuu”

Mshauri wangu alizungumza kwa sauti ya upole huku akinirazama usoni mwangu.

“Camel ana kwenda kuwa raisi wa Israek huoni kama wewe ukiwa raisi wa hii nchi muta saidiana kwenye mambo mengi, ikiwemo kuhakikisha hawa Scorpion muna waangusha. Hembu fikiria hilo ndugu yangu”

“Naomba unipe muda nikajadilane na wanangu kwanza kama wakihitaji nigombanie basi nita gombani aila kama hawato hitaji basi sinto gombania”

“Nashukuru sana ndugu yangu”

Tukatoka katika ofisi hii ya vioo.

“Kuna ndege yoyote nyingine ya jeshi iliyo tumwa?”

“Hakuna muheshimiwa raisi”

“Naomba tsikilizaje viongozi wote wa majeshi. Endapo kuna ndege ya aina yoyote iwe ya abiria jeshi itaingia nchini mwetu pasipo kufwata sheria na wakashindwa kujitabulisha wao wenyewe basi nina toa idhini ya kuziangusha ndegi hizo. Anga letu sio anga la kuchezewa kwamba kila anaye hitaji kupita basi apite. Tuna elewana?”

“Ndio kmuheshimiwa raisi”

“Alfajiri njema”

“Nawe pia muheshimiwa raisi”

Nikatoka kwenye ukumbi huu.

“Ruben”

“Ndio muheshimiwa”

“Nenda kapumzike. Umefanya kazi kubwa”

“Nashukuru muheshimiwa raisi”

“Nikikuhitaji nitakupigia simu”

“Sawa muheshimiwa raisi”

Nikaachana na Ruben na kuelkea ninapo ishi huku mwili wangu ukiwa umejawa na uchovu mwingi. Nikamkuta Cautrher akiwa amelala pamoja na mwanaye, nikawatazama kwa sekunde kadhaa kisha nikatoa simu yangu mfukoni, nikawapiga picha kadhaa kisha nikapanda kitandani.

“Umerudi”

Cauther alizungumza kwa sauti ya uchovu.”

“Ndio mke wangu”

“Mwanao alikuwa an analia lia hivyo nikaona nilale naye hapa. Amenyonya hapa na usingizi umempitia jumla”

“Ila asante sana mke wangu”

“Asante ya nini mume wangu?”

“Umenipatia mtoto mzuri sana”

“Hahahaa ni jukumu langu hili mume wangu. Nipo tayari kukuzalia hata watoto kumi”

“Kweli?”

“Haki ya Mungu vile ni wewe na uhitaji wako. Ukitaka hata kumi na kama Mungu akipa hao kumi nita kuzalia”

Nikampiga busu Shamsa kidogo.

“Nikiachia madaraka sijui hii inchi ita kuwaje?”

“Kwa nin una sema hivyo mume wangu?”

“Nasema tu kwa sababu naona kama kutakuwa na giza huko mbeleni”

“Usijali mume wangu, kama Mungu amekuongoza na umeifanya kazi yako basi atamuongoza huyo anaye kuja. Wala usiwe na mashaka kwa maana wewe sio raisi wa kwanza kuwepo hapa nchini”

“Sawa mke wangu, vipi bado una hitaji kubaki hapa nchini au?”

“Hapana mume wangu. Nimeona tukaishi mbali nah ii nchi”

“Sawa mke wangu, ngoja nilale kidogo. Saa mbili niamshe”

“Sawa baba Nadia”

Hazikupita hata dakika kumi usingizi ukanipitia.

“Mmmm honey hembu amka huku”

Sauti ya Cauther ikanifanya nifumbue macho na kumtazama.

“Niambie mke wangu”

“Ona kuna ajali imeitokea. Lori la mafuta limelipuka na wananchi wameteketea kwa moto”

“Imetokea wapi?”

Nilizungumza kwa sauti iliyo jaaa mikwaruzo ya usinfgizi.

“Tabora?”

Cauther akanikabidhi simu yake na nikatazama picha za wananchi wengi walio ungua kwa moto. Usingizi na uchovu wote ukakatika.

“Mungu wapi. Imetokea saa ngapi?”

“Imepotiwa na hii website ya habari dakika kumi zilizo pita”

“Imekuwaje wakafariki?”

“Munadishi ana dai kwamba hilo lori lilianguka hivyo watu wakakimbila kuchota mafuta, sasa limelipuka na picha ndio kama hizo”

Simu yangu ikaanza kuita, nikiachukua na kuona ni namba ya mshauri wangu mkuu.

“Muhehsimiwa raisi kuna ajali kubwa imetoka”

“Hii ya lori”

“Ndio”

“Aisee, ndio mke wangu ana nionyesha hapa”

“Nakutumia picha za tukio zima”

“Sawa nitumie na wasiliana na mkuu wa mkoa wa Tabora muambie aniandalie ripoti nzima ya ajali hiyo na hadi sasa wana sadikika wamefariki watu wangapi?”

“Si chini ya sabibi”

“Mungu wangu. Ukozi umefikia wapi?”

“Vyombo vya uokozi vimefika eneo la tukio ila kama unavyo jua predroli mkuu”

“Aisee majerui je?”

“Wanaendelea kuokolewa. Idadi kamili bado hajapatikana”

“Imetokea Tabora eneo gani?”

“Nzega karibu na stendi hivyo vijana wengi waendesha pikipiki ndio wamekubwa na mkasa huo kwani walikuwa wengi wakichua mafuta”

“Mmmm kazi kweli kweli”

“Mkuu huu ni msiba wa taifa ina bidi ulitanagazie taifa siku za maombolezi”

“Ngoja kwanza ukoaji umalizike, tujue walio fariki ni wapangapi walio majeruhi ni wangapi baada ya hapo tutatangaza siku za maombolezo. Alafu mkuu wa kitengo cha zima Moto muambie aje ikulu sasa hivi”

“Sawa muheshimiwa raisi”

“Usimshau na IGP”

“Sawa muheshimiwa”

Nikakata simu huku Cauther akiunitazama machoni mwangu.

“Tuna fanya nini mume wangu?”

“Hata sijui mke wangu”

“Mmmmm, au iliegeshwa hilo gari na maadui zako?”

“Kama ilikuwa ni ajalki ya kawaida basi ni mapenzi ya Mungu. Ila ni kama ajali ya kupangwa baada ya uchunguzi tuta jua nani muhusika”

“Sawa mume wangu.”

Nikaoga na kupata kifungua kinywa kisha moja kwa moja nikaeleka ofisini kwangu.

“Muheshimiwa IGP na mkuu wa jeshi la zima moto wamesha fika.”

Mlinzi wangu mwengine alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.

“Waambia waingie”

“Sawa mkuu”

Nikasimama katikati ya ofisi hii na kuitazama, kisha nikaka kwenye kiti kimoja huku nikiwa na mawazo mengi. Mlango ukafunguliwa na mlinzi wangu na akachungulia.

“Wamefika muheshimiwa raisi”

“Waambie waingie”

IGP pamoja na mwezake wakaingia ofisini hapa. Wakanipigia saluti na wakaka kwente viti vilivyopo mbele ya ofisi yangu hii. Nikawasha tv na sote tukaitazama habari inayo rushwa mubashara kutokea Tabora.

“Nani anapaswa kuwajibika kwenye hiyo ajali?”

Swali langu likawafanta wazee hawa kukaa kimya kwa sekunde kadhaa huku akitazamana.

“Aahaa muheshimiwa raisi ajali ilitoa kwa uharakakabla ya vyombo vya ulinzi kufika eneo la tukio”

IGP alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.

Nikanyanyua mkonga wa simu yangu ya mezani, nikaingiza namba ya Willy na nikampigia.

“Kaka”

“Upo wapi?”

“Nipo nyumbani na mama kijacho, tunaangalia hii ajali iliyo tokea”

“Hembu jaribu kufwatilia kwa satelaite uniambie ni muda gani hadi gari limeanguka, watu walivyo chota mafuta na hadi mlipuko ulivyo tokea”

“Sawa kaka dakika tano”

“Poa”

Nikakata simu, nikaona kifua cha IGP kikipanda taratibu ikidhihirisha ana wasiwasi. Ukimya ukatawala ofisini hapa huku viongozi hawa wakionekana kujawa na hofu kubwa sana. Baada ya dakika tano Willy alanipigia kwa simu yangu ya kawaida.

“Ndio”

“Upo ofisini kwako?”

“Ndio”

“Naituma kwenye hiyo tv yako”

“Sawa sawa”

Nikabadilisha mfumo wa tv hii na kuingia katika mfumo wa email. Nikafungua video hii na tukaanza kuitazama. Tukashuhudia jinsi lori linavyo aguka huku dereva wa lori huyo akijiatahidi kumkwepa bodaboda na gari ikamshinda na ikaanguka. Tukaona jinsi wananchi wanavyo livamia lori hilo huku wengine wakiwaokoa dereva na msaidizi wake huku wengine waking’ang’ania mfuniko wa tankio la mafuta na wakafanikiwa kufungua na wakaanza kugombania mafuta hayo kana kwamba wana gombania chakula. Uchotajiwa mafuta hayo.

“Eneo hilo si lina kituo cha polsi?”

“Ndio muheshimiwa”

“Wameshindwa kuzuia watu kichota mafuta au nao wamepandikiza vijana wao wawachotee dungu mbili tatu?”

Wazee hawa wakakaa kimya, Nikaipelekea mbele video hii hadi eneo gari lilipo lipuka.

“Imechukua lisaa zima na dakika kumi na sita, polisi mupo, zima moto mupo, na hadi watu wana anza kuungua hapo imechukua dakika ishirini kwa zima moto kufika. Kwa nchi kama hii, yenye kila aina ya uwezo wa kiuchumi, kisilaha na nahisi sidhani kama kwenye vituo vya zima moto kuna gari chakafu hata moja. Askari na zima moto mulishindwa nini kuwahi kufika eneo la tukio mapema?”

Swali langu likawafanya wakuu hawa kukaa kimya”

“Huu ni uzembe wenu, nyinyi na vikosi vyenu hamjui kazi ya kufanya. Dunia nzima sasa ina shangazwa na uzembe huu. Bora lingekuwa limeangukia porini huko mungesema ni porini. Hapo Nzega kabisa si mjini tena karibu na stendi, alafu polisi na zimamoto wamkekalisha makalio yao maofisini. Hivi si kila ofisi zenu zina mifumo ya kupata habari ya tukio la uhalifu na ajali kwa uharaka si ndio”

“Ndio muheshmiwa”

“Imekuwaje ikiwa tumewazesha kwa kila aina ya uwezo. Nchi namba moja duniani kwa utajiri na nguvu, tumempiga chini Mmarekani, ila mumezubaa kweli, au mulusubiria wananchi wawapigie simu, kuna ajali, ikiwa wenyewe walikuwa wana jua kwamba eneo hiloi ndio la wao kutoka kimaisha wakipata dungu za mafuta”

Nilizungumza kwa kufoka sana.

“Muheshimiwa raisi nina kuomba utusamehe”

“Alafu nikiwasamehe roho za hao watu wasio na hatia zita rudi, Wataendelea kuwa haina kupumua si ndio?”

Wazee hawa wakaka kimya.

“Nahitaji askari wa zima moto, askari walio kaa control room kwenye mkoa wa kipolisi Tabora, wawajibishwe haraka iwezekanavyo kwani uzembe wao sasa hivi nchi ime ingie kwenye midomo ya vyombo vya habari. Muna nielewa?”

“Ndio muheshimiwa raisi”

“Sasa uzembe huu utokee tena, mutalijua jina la mama yangu alikuwa ni nani. Munaweza kwenda”

Nilizungumza kwa ukali na wazee hawa wakasimama, wakanipigia saluti huku wakiwa na wasiwasi. Sifa moja ya kiongozi ni yule anaye hakikisha ana simamia misingi na taratibu iliyo wekwa hata kama aliye vunja sheria ni mtu mzima au ndugu yako hakuna haja ya kumpendelea wala kumuogopa. Nikashusha pumzi nyini, nikamimina maji katika glasi na kunywa glasi nzima kuhakikisha kwamba hasira yangu ina pungua kwa kisi kwani hii ndio tiba yangu ninapo kuwa na hasira. Nikanyanyua mkonga wa simu ya mezani na kumpigia mkuu wa mkoa wa Tabora.

“Muheshimiwa raisi habari yako”

“Sio nzuri, mumefikia wapi kuwaokoa hao wananchi”

“Muheshimiwa raisi kusema kweli uokoaji una endelea vizuri ila walio fariki ni wengi sana hadi sasa hivi sijajua idadi yake mkuu. Ila nikifahamu idadi ya walio kufa na walio jeruhiwa nita kujulisha”

“Nashukuru na nina subiria ripoti kutoka kwako”

“Sawa muheshimiwa raisi”

Nikakata simu na kushusha pumzi nyingi sana, kila chaneli ninayo iweka ina onyesha maswala ya msiba. Nikajikuta nikizima tv hii, mlango wa ofisini kwangu hapa ukagongwa.

“Ingia”

Akaingia mshauri wangu mkuu.

“Muheshimiwa raisi”

“Naam”

“Kuna tatizo moja limetokea?”

Mshauri wangu alizungumza kwa sauti moja huku akinitazama kwa macho yaliyo masikitiko jambo lililo nifanya kushusha pumzi kwani kama ni tatizo jengine limetokea basi siku ya leo ni balaa tupu kwenye hii nchi.

“Kuna nini?”

“Kuna moja ya kanisa waumini wake wameuliwa kwa bomu la sumu na waumini zaidi ya mia tano hamsini waumeuwawa”

Nikajihisi utumbo wangu ukinicheza kwa presha kwani katika siku moja kupoteza idadi kubwa ya wananchi sio jambo rahisi.



Kajasho kakaanza kunichuruzika usoni mwangu, mapigo ya moyo yakaanza kunienda kasi kwani hii sio kawaida. Nikafungua vifungo viwili vya juu vya shati langu huku nikitafakari nini cha kufanya.

“Imetokea wapi?”

“Kawe, mkuu”

“Imekuwaje?”

“Kulikuwa na ibada ya maziko ya mtoto wa mchungaji mkuu wa kanisa hilo. Alifia Afrika kusini alikuwa na Cancer ya ubongo, sasa leo kuliwa na ibada ya kuuaga mwili wa Marehemu, hivyo sumu hiyo imeingizwa kwa kupitia bomba za AC zilizopo kanisani”

“Ni sawa na walicho kifanya kwa raisi kule Ujerumani?”

“Ndio mkuu na sumu ni kali sana kwani imewaua ndnai ya dakika”

“Niandalie msafara nahitaji kwendan eneo hilo”

“Sawa muheshimi raisi”

Nikanyanyuka na kutoka ofisini kwangu moja kwa moja nikaelekea nyumbani kwangu, nikamkuta mke wangu pamoja na mdogo wake wakiwa wamekaa sebleni huku wakitazama habari ya mauaji yaliyo tokea, taratibu Cauther akanyanyuka na akanikumbatia kwa hasia kali kwani huu ni msiba wa taifa.

“Pole sana mume wangu”

“Nashukuru mke wangu. Nahitaji kuelekea eneo la tukio”

“Sawa mume wangu kuwa makini”

“Sawa”

“Shem pole kwa mana hii sio hali ya kawaida”

“Nashukuru”

Tukaingia chumbani na Cauther, akaniandalia nguo za kuvaa. Nikaoga na kurudi chumbani.

“Ni kina nani wamefanya haya mauaji?”

“Naamini upelelezi una fanyika ila adui tuta mbaini”

“Sawa mume wangu. Mungu akutangulie”

“Nashukuru mke wangu”

Nikambusu Cauther katika lipsi zake kisha nikambusu na mtoto wetu aliye lala kitandani na nikatoka ndani hapa. Nikamuaga shemeji na nikatoka ndani hapa na walinzi wangu wanne wakanizunguka, wawili wakiwa mbele huku wawili wakiwa nyuma. Nikafika katika gari la raisi, nikafunguliwa mlango na nikaingia ndani, mshauri wangu naye akaingia upande wa pili wa gari hili na msafara ukaanza.

“Una hisi ni kina nani wamefanya hivi?”

“Watakuwa ni Scorpion mkuu kwani kifo hichi hakitofautiani na kifo cha raisi”

“Hawa jamaa sijui niwafanye nini?”

“Tatizo ni kwamba tuna kula nao, tuna amka nao na tuna shinda nao. Ila wangekuwa wana julikana kirahisi mkuu mbona tungekuwa tumesha waua”

Simu yangu ikaanza kuita nikaitoa mfukoni na kuona private namba. Nikaipokea na kuiweka sikiooni mwangu.

“Heloo EDDY”

Niliisikia sauti ya makamu wa raisi.

“Una hitaji nini?”

“Sina ninacho kihitaji ila nimekupa taarifa kwmaba usingaishe wapelelezi kupeleleza juu ya mauaji hayo ya kanisani. Nimefanya kwa kulipiza mauaji ya mpenzi wangu Caro. Hivyo enjoy na msiba huu”

Simu ikakatwa na nikajikuta nikitetemeka kwa hasia.

“Mkuu vipi?”

“Ni makamu wa raisi. Amekiri kuhusika na haya mauaji ili kulipiza kisasi cha mpenzi wake Caro”

“Shenzi sana huyu mpuuzi”

“Nisikilize mzee wangu. Nahitaji ugombanie uraisi kwa ajili yangu, tafadhali nakuomba”

Mshauri wangu akanitazama kwa sekunde kadhaa kisha akatingia kichwa akimaanish kwamba yupo tayari kugombania uraisi.

“Nitakuwa raisi wa hii nchi nita hakikisha huyu mshenzi nina muwinda ipasavyo”

“Nashukuru sana, tena sana na sasa nita kuwa na amani kubwa sana kama nitaicha nchi mikononi mwako.”

“Mungu abariki wananchi wanikubali kwa maana ni lazima hawa Scorpion wana weza kukiunga chama chochote ili mradi waweke mtu wao”

“Tuta pambana na sisi ndio serikali. Hata kwa kuiba kura, uta ingia madarakani”

“Sawa”

**HAYA SASA KILE KIGONGO AMBACHO MULIKUWA MUNA KISUBIRIA KWA HAMU AIIISSII YOU KILL ME CHAPTER FOUR(Killer) sasa itapatikana kupitia group la whatsapp kuanzia 12/08/2020 kupitia whatsapp na facebook private group. Kwa maelezo zaidi wasiliana nami 0657072588 au 0742334453. ADA YA GROUP NI SH 4000 TU KWA MWENZI AU TEMBELEA PAGE YANGU YA FACEBOOK Story Za Eddy-tz KWA MAELEZO ZAIDI. KARIBU SANA)**

Tukafika eneo lilipo tokea tukio. Tukakuta ulinzi ukiwa ni mkali hukuw ananchi wakiwa wamezuiwa kulikaribia eneo hli. Kioo kinacho nitenganisha na dereva wangu kwenye hili gari, kikafunguliwa.

“Muheshimiwa raisi tuna omba utulie kwanza hadi tuhakikishiwe usalama wa hali ya hewa”

“Sawa”

Nikaona waandishi wa habari wengi walio kaa kwa mbali jinsi wanavyo endelea kurusha kila kinacho endelea eneo hili. Wataalamu wanao toa maiti hizo wamevalia mavazi maalumu kama watu wanao shuhulika na wagonjwa wa Ebola.

“Matizi hazijatolewa zote?”

“Ndio muheshimiwa raisi kwa maana watu mia tano na ushee sio wachache aisee”

“Duuu”

“Ila hivi vifo ipo siku ata lipa”

Mshauri wangu alizungumza huku akitetemeka mikono yake kwa hasira. Nikatazama jinsi maiti hizi zilivyo wekwa kwenye plastic beg maalumu za kubeba maiti.

“Muheshimiwa raisi ina bidi uvae hichi”

Mlinzi wangu alinikabidhi kifaa malumu cha kunisaidia kuzuia kuvuta hewa chafu. Akamkabidhi na mshauri wangu na sote tukavivaa huku vikiziba pua na midomo yetu. Nikaruhusiwa kushuka ndani ya gari, nikapokelewa na waziri wa mambo ya ndani ambaye alifika eneo hili kabla yangu.

“Karibu sana muheshimiwa raisi”

“Asante”

Nilizungumza huku nikiona maiti za watoto wadogo huku wenginne wakiwa ni vichanga kabisa. Hali hii ikanifanya machozi kunilenga lenga huku hasira ikinipanda kisawa sawa.

“Nahitaji kuingia kanisani”

“Sawa muheshimiwa raisi ina bidi uvae vazi hili”

Nikavalishwa vazi moja kama hawa wanao endelea na hali ya kuokoa maiti hizi. Walinzi wangu wanne nao wkaavaa mavazi haya na taratibu tukaingia katika kanisa hili kubwa.

‘Mungu wangu?’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikitazama maiti zilizo lala na kwa bahati mbaya hili kanisa ni kanisa la gorofa moja kama vile ukumbi wa sinema. Wengine wamefariki huku wakiwa wamekumbatiana, wengine wakiwa wameshikana mikono. Nikajikuta nikisimama mara baada ya kumuona binti mdogo aliye valia geuni jeusi huku akiwa amesuku vizuri rasta zake. Kwa kumkadiria ana miaka isiyo zidi kumi. Binti huyu akanifanya machozi kunichuruzika na nikashindwa kujizuia kabisa kwa maana amekufa kifo ambacho hakupaswa kufa na mdogoni mwake. Taratibu nikamnyanyua.

“Muhehsimiwa raisi acha tu tuta shuhulika”

Muokoaji mmoja alizungumza, nikamtazama kwa jicho moja kali na kuwafanya walinzi wangu kumsogeza pembeni, nikaanza kutemeba na binti huyu huku akiwa amelegea kabisa mikono mwangu.

‘Je angekuwa ni Nadia wangu, ningefanya nini?’

Niliwaza kichwani mwangu huku nikiendelea kulia kwa uchungu mwingi sana.

Nikamkabidhi biti huyu kwa wanao weka maiti hizi ndani ya mabegi ya plastiki yenye zipu. Nikakaa kwenye moja ya bechi la hapa kanisani huku nikitazama namna uokoaji unavyo endelea.

‘Eddy hukuletwa duniani kushuhudia haya. Umeletwa kuwasiadia wasio na uwezo. Kumbuka umezaliwa kuwa yatima hujui baba wala mama. Ndugu zako ulio kua nao wame uwawa. Hawa walio lala hapa ndio ndugu zako. Ina bidi ufanye jambo’

Niliisikia sauti moja ikinisemesha moyoni mwangu.

‘Wamekufa wakiwa wamekuja kumuaga ndugu yao aliye fariki ila wao wamejumuika nao kwenye hichi kifo. Hawakupaswa kufa. Fanya jambo Eddy’

Sauti hiyo iliendelea kuzungumza na mimi. Nikasimama na kuanza kutembea kuelekea mbele, nikafika eneo lenye msalaba mkubwa.

‘Mungu kwa nini umewaacha wamekufa ndani ya nyumba yako, kwa nini umewaacha wameshindwa kujitetea japo kwa kutoka nje. Kwa nini kukuwaonyesha kwamba kuna kifo kina kuja mbele yao, ila umesababisha ndoto za mamia zime kufa kwa ajli ya mtu mmoja eheee?’

Nilizungumza kimoyo moyo ila kwa uchungu wa hali ya juu.

‘Ona watoto wadogo, wengine ni wachanga kabisa, hawajaweza hata kuita mama. Wamekosea nini huyu binadamu, kwa nini usimpige hata radi moja akafa akaacha kutenda haya maovu eheee?’

Niliendelea kulalama huku nikilia kwa uchungu.

‘Ulinipa huu uraisi ili nishuhudia haya, eheeee. Ulinifanya niwe kiongozi wa hawa watu ili iweje, mimi ni kiongozi wa aina gani? Kiongozi ambaye nina shindwa kuwalinda watu wangu, ninawaacha wana kufa mamia kwa ajili ya mpuuzi mmoja. Ni wapi nimekukosea Mungu, kwa nini wasife wengine watu wabaya hadi wafe watu hawa, kweli Mungu upo na kusikia hichi ninacho kuomba, eheee?’

Nilizungumza kwa uchungu mwingi sana hadi nikajikuta nikipiga magoti chini na kuendelea kulia kwa uchungu wa hali ya juu.

‘Mungu kama una nisikia niambie nini nifanye ehheee?’

Niliendelea kulalama kimoyo moyo.

“Muheshimiwa”

Niliisikia sauti nyuma yangu, nikageuka taratibu na kumkuta mshauri wangu akiwa amesimama huku naye akiwa amevalia mavazi kama haya. Akanipa mkono wake wa kulia nikautazama kwa sekunde kadhaa kisha nikaushika na akaninyanyua. Akanitazama jinsi machozi yanavyo nimwagika na kwa bahati mbaya siwezi kuyafuta kwani nguo hii eneo la kichwani lina kitu kama helment ngumu ambayo ina kioo kikubwa.

“Una takiwa kuwa jasiri, una paswa kuwa mkakamavu. Wewe ndio una tuongoza kwa sasa, endapo uta kuwa mnyonge una hisi sisi ita kuwaje kwa upande wetu?”

Mshauri wangu alizungumza huku akinitazama na mkono wake wa kulia akiwa amenishika begani.

**HAYA SASA KILE KIGONGO AMBACHO MULIKUWA MUNA KISUBIRIA KWA HAMU AIIISSII YOU KILL ME CHAPTER FOUR(Killer) sasa itapatikana kupitia group la whatsapp kuanzia 12/08/2020 kupitia whatsapp na facebook private group. Kwa maelezo zaidi wasiliana nami 0657072588 au 0742334453. ADA YA GROUP NI SH 4000 TU KWA MWENZI AU TEMBELEA PAGE YANGU YA FACEBOOK Story Za Eddy-tz KWA MAELEZO ZAIDI. KARIBU SANA)**

“Pambana”

Nikatingisha kichwani kimaanisha kwamba nime muelewa. Nikaanza kutembea kuelekea nje, tukatoka nje na tokaombwa kuingia kwenye moja ya hema. Tukapuliziwa dawa maalumu ya kuua backteria watokanao na sumu hii. Baada ya zoezi hili tukavuliwa mavazi haya na moja kwa moja nikaingaia ndani ya gari.

“Saa tisa kamili alasiri nahitaji kuhutubia taifa”

“Sawa muheshimiwa raisi”

Nikatazama saa yangu ya mkononi na sasa hivi ina onyesha ni saa nane kasoro mchana. Tukafika ikulu na moja kwa moja nikaeleka ofisini kwangu.

“Kauli ya makamu wa raisi aliyo sema kwamba amelipiza kisasi cha kifo cha Caro kwa kuua mamia ya watu ikanifanya nikasirika snaa.

“Kjhaargrrahahaaa……”

Nilizungumza kwa hasira huku nikichangua vitu vyote vilivyopo juu ya meza hii na vikaanguka chini, jambo lilio wafanya walinzi wangu kuingia kwa haraka ofisini hapa.

“Mkuu vipi?”

Waliniuliza huku wakinitazama kwa mshangao.

“Nipo salama musijali, nahitaji kuwa peke yangu sasa hivi”

“Sawa mkuu”

Wakanitazama kisha wakatoka ndani hapa. Kila ninapo jaribu kukaa nahisi kama moyo wangu una nienda kasi. Mshauri wangu akaingia ndani hapa, akashangaa kidogo kupona vitu vilivyokuwa juu ya meza yangu vyote vikiwa vimeanguka chini.

“Nimesha andaa muheshimiwa raisi”

“Saa tisa bado?”

“Bado nusu saa. Ila mkuu hujaandaa speech yoyote?”

“Ipo hapa”

Nilizungumza huku nikimuonyesha mshauri wnagu kichwa changu.

“Ila mkuu”

“Niamini”

“Sawa muheshimiwa raisi”

Tukaka ofiisni hapa hadi saa tisa kasoro dakika tano nikaeelekea kwenye eneo maalumu ambalo raisi hutumia kwa ajili ya kuhutubia wananchi. Nikakuta kamereza zikiwa zimeshaa andaliwa.

“Mkuu make up?”

Binti anaye shuhulika na maswala haya alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.

“Siendi kuwatangazia wananchi kwamba nina wapandishia misharaha. Hivyo hakuna haja ya make up”

Nikasimama katika eneo hili huku nikiwatazama watu walimo eneo hili.

“Tatu, mbili, moja upo hewani muheshimiwa raisi”

“Ndugu Watanzania, ni masikitoko makubwa, kuwapoteza ndugu zetu wapendwa. Shambulizi lililo tolea leo asubuhi kanisani. Ni shambulizi la kigaidi. Shambulizi ambalo lina ua mamia ya watu waiso na hatia. Watu ambao walikwenda kanisani pale kwa ajili ya kuaga mwili wa mpendwa woa ila wao wameungana nao”

Nilizungumza kwa sauti ya upole na iliyo jaa msisitizo mkali.

“Tukiwa kama taifa hili lililo tokea leo hatuwezi kukaa kimya au kuliacha lipite. Nina waaapia kwa maisha yangu, nipo tayari kufa kwa ajili ya kuitetea hii nchi na wananchi waliomo ndani yake.”

Nikanyamaza kidogo kisha nikaendelea kuzungumza.

“Wahusika wakuu wa hili tukio ni Scorpion. Niwaambie Scorpion wote mulipo hapa Tanzania na nje ya Tanzania, nina wawinda, nita wawinda na nita hakikisha mmoja baada ya mwengine muna kufa kwani najua ni wapi mulipo, nini muna fanya na kipi muna panga baada ya hili. Jipangeni”

Baada ya kumaliza kuzungumza manebo haya kwa uchungu wa hali ya juu nikaondoka eneo hili na kuwaacha watu wote wakiwa kimya kwani walitegemea nita zungumza maneno mengi ila nimezungumza machache na yana eleweka.



“Mkuu mkuu”

Mshauri wangu aliniita na nikapunguza mwendo wa kutembea na tukawa sawa.

“Muheshimiwa raisi ndio umemaliza?”

“Ningekuwa sija maliza wala nisinge kuwa hapa”

Nilizungumza huku nikiendelea kutembea kwa mwendo wa kawaida na nikaingai ofisini kwangu.

“Ila muheshimiwa raisi wafiwa wa ajali ya lori walipaswa kusikia neno la faraja kutoka kwako muheshimiwa”

“Hili la mlipuko sidhani kama ni la muhimu sana kuliko hili tukio la kihaidi. Wale watu walikuwa kanisani wakisali, wakimuomba Mungu wakauwawa. Ila hawa walifwata roli wenyewe na yamewakuta”

“Sawa muheshimiwa raisi ila wote wale ni binadamu na wana haki sawa. Wewe ni kiongozi wa taifa endapo uta weka tabaka la nani amekufa kwa sababu gani hilo sio jambo zuri”

Mshauri wangu alizungumza kwa msisitizo huku akinitazama usoni mwangu.

“Wali walio kufa kwenye mlipuko kuna wamama, wanaume, vijana na wazee. Wote walifwata mafuta kutokana na uhitaji wa mafuta hayo. Ila tukiachana na hayo wote ni Watanzania na wana paswa kuzikwa kwa heshima kama Watakavyo zikwa hawa walio fia kanisani. Tafadhali nina kuomba uende tena hewani tafahdli muheshimiwa raisi”

Nikashusha pumzi nyingi sana huku nikimtazama mshauri wangu.

“Tafadhali mkuu nakuomba”

“Namuhitaji mke wangu”

“Sawa nina kwenda kumuita”

Mshauri wangua katoka eneo hili, nikatazama vitu hivi jinsi vilivyo pangwa kama vilivyo kuwa. Nikajiinamia katika meza, hazikupita dakika tano mke wangu akaingia ofisini hapa, nikasimama na kumkumbatia kwa nguvu.

“Vipi mume wangu”

“Naomba utupishe”

“Sawa muheshimiwa”

Mshauri wangu akatoka ndani hapa.

“Una tatizo gani mume wangu”

“Umetazama hotuba niluyo zungumza?”

“Ndio baby”

“Eti nimekosea kuzungumza vile?”

“Nani kasema umekosea mume wangu. Umepatia kwa asilimia mia moja kwa maana ni hotuba fupi na ya kueleweka”

“Eti sijawataja watu walio kufa kwenye ajali ya mlipuko wa lori je nimefanya kosa?”

“Huja fanya kosa mume wangu. Ila umesahau kuwahusisha kwenye hotuba hii. Una jua wewe ni kiongozi mzuri. Kiongozi ambaye ukitoa neon lako la faraja watu watafarijika. Hivyo mume wangu nina kuomba sana kama ina wezakana ila sijui, ila kama ina wezekana naomba nao uweze kuwatolea hutuba fupi japo nao wahisi kiongozi wao wa nchi ume guswa na matatizo yao”

“Niwaambie nini?”

Cauther akakaa kimya kwa sekunde kadhaa huku akinitazama usoni mwangu.

“Waambie umeguswa sana na ajali iliyo tokea na waambie kila familia iliyo poteza mwana familia basi ita patiwa pole kwa aina yake. Japo sio vyema kutaja kiwango cha kuwapa ila kma serikali ita jitolea kushuhulika na mazishi kwa wale ambao miili yao haito fahamika na wale ambao miili yao ita fahamika na wana ndugu kwa kupimwa labda DNA basi mazishi kama ni majeneza au sanda zita nunuliwa na serikali”

“Asante mke wangu kwa maana hapa akili yangu ilisha vurugwa yanai nime kwenda na kuona watoto wadogo, wengine wachanga kabisa wakiwa wameukufa pale kanisani. Roho imeniuma san make wangu, niliwahi kuwalilia wezangu tu wakiwa wamekufa na kile kilo leo hii ndio kimejirudia mke wangu nime umia sana”

“Najua mume wangu, pole sana ila nina imani kwanbu Mungu ata kutia nguvu kwenye hili na uta fanikiwa tu”

“Amen”

Cauther akanikumbatia kwa sekunde kadhaa.

“Naomba ukawafariji”

“Twende wote”

“Sawa”

Nikamshika mkono Cauther na tukatoka ndani hapa.

“Waambie nina kwenda hewani tena”

“Sawa mkuu, nina shukuru”

Mshauri wangu akawajulisha wanao dili na maswala ya mawasiliano na moja kwa moja tukaeleka hadi kwenye eneo la mawasiliano.

“Ngoja nikupake make up mume wangu”

Cauther akachukua vifaa vya binti anaye shuhulika na maswala hayo, akanipaka make up kidogo.

“Naamini uta zungumza yaliyo mazuri”

“Nashukuru mke wangu”

Cauther akaninyonya denda kidogo kisha nikasimama katika eneo nililo kuwa nimesimama. Kamera zikawashwa.

“Tatu, mbili, moja. Upo hewani muheshimiwa raisi”

“Ndugu zangu Watanzania, ninatoa pole kubwa sana kwa wafiwa walio pata ajali ya kuungua kwa mlipuko wa lori iliyo tokea Nzega mkoni Tabora. Kwa kweli ni vifo vya kuumiza na kusikitisha sana. Nikiwa kama raisi wa jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, nimeguswa na msiba huu, niwahakikishie wafiwa wote. Serikali yangu ita hakiisha kwamba ina wahudumia maziko ya ndugu zetu hawa wote, kuanzia mazishi, pamoja na misiba. Kila kaya itakayo tambua mwili wa ndugu yao basi serikali ita simamia maziko hayo huku wale ambao hawato tambulika basi nao serikali ita simamia. Serikali yangu ita toa rambirambi kwa kila familia iliyo ondokewa na mpendwa au wapendwa wao.”

Cauther akanionyooshea dole gumbaa akimaanisha kwamba ame kubali speech yangu.

“Jambo moja ambalo nina woamab ndugu zangu Watanzania. Nina waomba sana inapo tokea ajali ya gari liwe la abiria au mizogo. Tafadhali tuwe tuna jiadhari sana kukusanyika eneo la ajali hiyo kuepuka kupata maafa kama yaliyo wakuta ndugu zetu. Ninge penda kuwakumbusha jeshi la zima moto pamoja na jeshi la polisi. Inapo tokea ajali kama hii, musikae sana maofisini na kuwaacha wananchi wana ingia kwenye dhahama kubwa kama hii ya leo. Muna vyombo vya kisasa vya kutambua ajali zote zinazo tokea ndani ya hii nchi, muna usafiri wa kila aina kuanzia helicopter, boti za majini pamoja na magari maalumu yanayo kwenda kwa kasi kubwa. Ningependa mujitoe sana pale ajali inapo tokea na hili lililo tokea leo Nzega basi lisijirudie”

“Baada ya kuzungumza hayo, nirudie tena kutoa pole zangu za dhati kwa wanafamilia na taifa kwa ujumla. Mungu inariki Tanzania na Mungu ibariki Afrika asanteni kwa kunisikiliza”

Nikapewa ishara ya kwamba kamera zimesha zimwa na taratibu nikashuka kwenye eneo hili.

“Jamani kama niliwakwaza kwa hali niliyo kuwa nayo pale awali nina omba munisamehe. Mimi nami ni binadamu nina pitia kila hali ambayo nayi huwa muna pita”

Baada ya kuwaomba msamaha wafanyakazi wangu hawa nikatoka ndani hapa.

“Umeongea viruzi sana mkuu”

“Nashukuru sana ndugu yangu, najivuani sana kuwa na huyu mwanamke kwa kweli ni wanawake wachache sana wenye akili kama za Cauther”

“Asante sana mume wangu na nitakuwa nawe bega kwa bega hadi kufa kwangu”

“Nashukuru mke wangu. Ndugu yangu nina kwenda kupumzika sasa hivi”

“Hakuna shaka muheshimiwa raisi”

“Saa mbili usiku andaa kikao na majenerali wote wa jeshi”

“Sawa mkuu”

“Ila hii kazi imekupendeza mke wangu”

“Kazi gani baby”

“Kuwa mshauri wa raisi”

“Hahahahaa mimi nimekushauri kama mume wangu na sio kama raisi”

“Nashukuru mke wangu kwa kubeba matatizo yangu?”

“Hii ndio maana pale kanisani tuliambia tutakuwa mwili mmoja. Maana ya kuwa mwili mmoja ndio hii. Ttizo lako ni langu na tatizo langu ni lako”

“Nashukur mke wangu tena nimekumbuka jambo”

“Jambo gani?”

“Nahitaji kuzungumza na baba mkwe wakati huu”

“Sawa mume wangu nami nime mmiss sana baba yangu”

Tukafika sebleni, nikampigia baba mkwe na kwa bahati nzuri akapokea.

“Asante sana Mungu mwangu umepiga simu. Nilikuwa nina hamu kubwa sana ya kuzungumza na wewe”

“Nami pia baba habari ya huko?”

“Aha nina mshukuru Mungu kwa kweli mazao yana endelea kunawiri, vipi mkeo na mjukuu wangu wana endeleaje?”

“Wanaendelea vizuri baba yangu nipo na Nadia na Cauther hapa”

“Aisee naomba nipige video call”

“Sawa ngoja nikupigie”

Nikampigia video call baba mkwe na akaanza kuzungumzana wanaye huku furaha ikitawala katikati yao. Hali iliyo tufanya tusahau mamatizo yetu kwa dakika kadhaa. Cauther akaingia chumbani ili kumuonyesha baba yake binti yetu aliye zaliwa. Baada ya kumaliza na wanaye nikachukua simu na nikaingia katika ofisi yangu ili kuzungumza naye maswala nyeti ambayo mabinti zake hawapaswi kufahamu.

“Ndio mwanangu”

“Nina imani umeweza kuona hotuba zangu?”

“Ndio nimeziona hususani ya kwanza nimevutiwa nayo”

“Nimewapa vitisho ila sijajua wapi nianzie”

“Kwani zile detais nilizo wapatia pale awali hazikusaidia?”

“Najua wata kuwa wana badilisha mifumo yao kila wakati ndio maana nahitaji kuwawinda kimya kimya, nikiwa nje ya uongozi”

Baba mkwe akashusha pumzi huku akinitazama.

“Una jua kwa jinsi mfumo wa Scorpion ulivyo tengenezwa ni kwamba una wakuu wengi sana kila nchi ina mkuu wake na ukiangalia nchi ni nyingi walizo weka makao yao, hivyo sijajua una hitaji kudili nao vipi”

“Nahitaji kumuua makamu wa raisi”

“Ukimuua yeye, tambua wata kuja kwa ajili ya familia yako yote. Je upo tayari kumpoteza mke wako pamoja na mwanao”

“Nita walinda baba”

“Eddy Eddy, Eddy mwanangu, scorpion ni wengi sana, tena sana. Wapo hadi waendesha bodaboda na bajaji”

“Hivyo kumbe?”

“Nakuambia ukweli, yaani ni kizazi kibaya sana tulicho kitengeneza. Ndio maana kwenye vita huto weza kupambana nao wote.”

“Una nishauri nini baba?”

“Ukiachana na uongozi, fanya maisha yako ya kawaida. Usiwaguse kabisa, uta pata tabu una binti mzuri sana na una mke mzuri sana. Fanya maisha yako ya kawaida kabisa”

“Je wakinifwata kwenye maisha yangu ya kawaida?”

“Wakikufwata hapa wata kuwa una haki ya kuwashambulia”

“Ila baba unavyo sema kwamba nita kuwa na haki ya kuwashambulia ikiwa leo wameuwa wamia ya watu katika kanisa, watu waiso na hatia kweli una hisi ni watu wa kusamehewa”

“Wana hitaji uwakabili ili wakupoteze Eddy mimi ni miomgoni mwa wale waanzilishi. Hivyo najua tulivyo panga taratibu na sheria zetu”

“Ndio maana walikuua na umekaa kimya na kujificha si ndio, umechukua hatua gani hadi sasa hivi kukabiliana nao ehee?”

Nilifoka kidogo na kumfanya baba mkwe kukaa kimya kidogo.

“Ni nini ulicho kifanya baba, niambie, ni nini ulicho kifanya?”

“Nina familia kubwa na wajukuu wengi, ndio maana sijahitaji kufanya chochote Eddy, Ila kama humpendi Cauther na mwanao basi washambulia ila kama una wapenda. Fwata ushauri wangu, sasa hivi ume gadhibika, hasira itakapo kwisha uta nipigia”

Baba mkwe akakata simu na nikashusha pumzi nyingi. Simu yangu ikaingai meseji kutoka kwa mshauri wangu mkuu.

‘Muheshimiwa sahamani kwa kukusumbua, Camel amesha ingia nchini Tanzania na nipo naye sasa hivi, nimpeleke hoteli au nije naye ikulu’

Nikampihia simu mshauri wangu.

“Ndio muheshimiwa raisi”

“Naomba umlete sasa hivi ikulu”

“Sawa mkuu”

Nikakata simu na nikatoka ndani hapa.

“Mume wangu chakula kipo tayari”

“Ni kingi?”

“Ndio nimepika cha kutosha najua hujakula chakula toka asubuhi”

“Sasa kuna mgeni kuna mwana mama ana itwa Camel ni miongoni mwa watu walio tusaidia tulipo kuwa kule Israel”

“Ohoo ana kuja hapa nyumbani?”

“Ndio mke wangu”

“Basi ngoja tuandae mazingira ya kumpoea mgeni”

“Sawa mke wangu”

Cauther akasiadiana na wafanyakazi wa ndani kuandaa chakula kwa haraka haraka. Baada ya dakika ishirini madame Cameel akafika ikulu na nikampokea imi na mke wangu.

“Anaitwa Cauther ni mke wangu. Cauther ana itwa madame Camel”

“Nashukuru kukufahamu madem”

“Nawe pia, Eddy mbona hujanitambulisha kwamba mimi ni mke wa mshauri wako”

“Hahaaa”

Sote tukachekea.

“Karibu sana nchini Tanzania”

“Nashukuru kwa kweli”

Tukaingia hadi tunapo ishi.

“Ikulu yako ni nzuri sana Eddy”

“Nahsukuru japo sio ikulu yangu. Nikimaliza muda wangu basi nina toka na mwengine ana chukua nafasi yake”

“Ni kweli ila anaye kaa sasa hivi humu ndani ni wewe hivyo hii ni ikulu yako kabisa”

“Nashukuru sana mama yangu. Najua ni jioni sasa hivi ila tumeandaa chakula maalumu mimi na mke wangu na ningependa ukaribie mezani huku tukiendelea kuzungumza mambo mawili matatu”

“Nashukuru sana Eddy”

Tukaka mezani sisi wanne. Tukajipakulia vyakula hivi vilivyo andaliwa kwa utaalamu wa hali ya juu.

“Naomba tusali kabla ya kula”

Cauther alizungumza na kutufanya sote kutulia.

“Mungu bariki chakula hichi tunapo kila kikatupe afya na nguvu katika miili yetu ya kuweza kukutumikia wewe ame”

“Amen”

Tuliitikia kwa pamoja.

“Aisee Eddy mwanangu”

“Ndio mama”

“Umepata chuma cha uhakika. Una mke mzuri sana”

“Nashukuru sana mama yangu”

“Cauther binti yangu”

“Ndio mama”

“Eddy ni mwanaume jasiri, kwenye maisha yangu ukimtoa huyo mume wangu niliye kaa naye hapa kuhsoto kwangu, basi Eddy ni mwanaume jasiri. Ameweza kutoka kwenye mikono ya wale washenzi kwa kweli nimeona ana kitu cha pekee ndani mwake, kitu ambacho ni mara chache sana kukipata kwa wanaume. Hivyo tulia na mwanangu”

“Nashukuru mama nami nina jivunia kuwa na mwanaume kama huyu. Aliweza kupigania penzi letu kindichi hicho akiwa ni dereva taksi hivyo nina muamini kwa maisha yangu yote na wala sinto kuja kukaa na kumuacha, nife mimi, afe yeye au tufe sote huo ndio utakuwa mwisho wa maisha yetu”

“Nafurahi kusikia hivyo. Ehee niambie mwanangu Eddy, una jua ombi lako lilinyima usingizi kabisa japo mimi ni muumini mzuri wa kulala”

“Hahaha pole sana mama yangu”

“Nashukuru kwa kweli kwa maana nimekaa nikatafakari, nikawaza nika chekecha akili yangu nikaseha hapana ngoja nionane na huyu kijana.”

“Pole kwa mara nyingine kwa kukupa mawazo mengi”

“Mimi nimesha poa. Nilimuuliza baba yako hapa hata yeye ameniambia hajui ni kwa nini uliniambia vile kwamba ni niipindue serikali yangu iliyopo madarakani. Hivyo nimekuja unipe sababu kwa nini niipindue serikali yangu?”

Nikashusha pumzi huku nikimtazama madame Camel usoni mwake kwa maana ina bidi nitume akili kubwa sana kumshawishi mwana mama huyu kumpindua raisi wake.



“Dunia kwa sasa ipo mikononi mwa kikundi kimoja kinacho itwa Scorpion naamini umekisikia?”

“Nakijua na mulisha niiambia na ndio wahusika na tatizo lililo tokea kule Israel”

“Ndio”

“Ehee”

“Raisi wako wa nchi yupo kwenye hicho kikundi pia na alisha pewa amri ya kuweza kunia. Ametumia nafasi aliyo kuwa nayo kuniua. Nimetafakari kama nikilipiza hili swala kama nchi lina weza kugarimu maisha ya wananchi wasio na hatia. Hivyo ningependa sana huyu raisi aondolea madarakani kabla ya muda wake”

“Una jua Eddy katika nchi yangu hilo swala ni gumu sana na kama unavyo jua japo nchi yetu ni sio maarufu sana kama yako na Marekani ila nchi yangu ina nguvu sana kutokana na zile ahadi ambazo Mungu aliziweka juu ya ichi yetu. Umebakisha muda gani kwa wewe kuwa madarakani?”

“Siku kadhaa”

“Nitakacho kusaidia labda ni kulipiza kisasi wewe kama wewe. Ila sio kwa kupindua serikali nzima”

“Sasa kama nikimuua mimi na ikijulikana dunia nzima ita kuja juu yangu?”

“Ndio nakuambia hii ishu imekaa vibaya sana”

“Kwa nini musifungue kesi”

Cauther alizungumza huku akitutazamaa.

“Kesi?”

Niliuliza kwa mshangao.

“Ndio kwa nini musifungue kesi ambayo ita wawezesha kumstaki huyo raisi kwa hayo yote aliyo yafanya hiyo ita kuwa njia rahisi ya kuonyesha dunia kwamba hukutendewa haki ulipo kuwa ndani ya nchi hiyo”

Nikashusha pumzi nyingi huku nikimtazama Cauther.

“Ni wazo zuri mkwe wangu. Una jua kesi kwlei ita weza kuonyesha ni namna gani nchi kama nchi yetu ya Israel iliyo leta uzembe kwa maisha ya raisi wa nchi ya Tanzania”

“Mzee wangu hapo ana mpango wa kugombania uraisi. Nina imani kwamba ata weza kulishuhulikia hili, mimi nita jitoa kwenye hili kwa sasa nahitaji kuishi maisha ya kawaida sana na mke wangu. Nahitaji kujua namna gani naweza kulea familia yangu na wakafurahia uwepo wangu kwenye maisha”

“Ni wazo zuri Eddy ila unaonekana kukata tamaa au nimekukatisha tamaa kwani nina imani ulitegemea kwamba tumpindue raisi”

“Hujanikatisha tamaa mama yangu. Hili swala nilikuwa nako kwa kipindi kirefu sana hivyo wala usihisi kwamba wewe ndio umenikatisha tamaa”

“Nashukuru kwa kunielewa. Alafu pole sana kwa misiba hii mizito”

“Tumesha poa ndio maisha ya maadui zetu”

“Muta fanikiwa wala usijali ndugu yangu. Una jua njia ya adui ni fupi ipo siku atapatikana na ndio uta kuwa mwisho wa kikundi hicho”

“Nashukuru mama yangu”

Tukaendelea kula chakula hichi cha jioni huku tukizingumza mambo mengi ya kimaisha. Baada ya chakula hichi madame Camel pamoja na mashauri wangu wakaondoka ikulu hapa na kuelekea nyumbani kwa mshauri wangu huyu.

“Una waza nini mume wangu”

Cauther aliniuliza huku tukiwa tumejilaza juu ya kitanda tukitazama dari ya chumba chetu.

“Huwa nahisi haya yote wanayo yafanya hawa Scorpion ni kutokana na mimi kuwa kiongozi. Wana amua kuwaua watu wasio na hatia ilimradi maisha yangu ya uongozi yawe magumu”

“Usijilamu mume wangu. Kikubwa ni kwamba umebakisha mwenzi na siku kadhaa. Utaachana nah ii kazi na uta kwenda kuishi maisha mazuri tu”

“Hembu naomba laptop mke wangu”

Nilizungumza huku nikikaa kitako kitandani. Cauther akashuka kitandani hapa, akachukua laptop iliyo kuwa katika meza ninayo itumia kufanta kazi za kiserikali kama ninapo kuwa chumbani hapa.

“Nataka kuangalia ni eneo gani tuta nunu katika hizi nchi mbili nitakazo zitaja”

“Nchi gani nan chi gani?”

“Japan na nchi ya pili wewe ndio uitaje kwa maana mimi nimependekeza hiyo Japan”

“Mmmmm mimi sehemu ninayo iona itakuwa ni salama kwa kuishi labda ni India”

“Mmm! Umechagua India kutokanana kwamba ndio chimbuko la mzee?”

“Hapana, ila India nina Marafiki zangu wengi sana na hali ya hewa ya India nina ifahamu vizuri na itakuwa ni nzuri kwa maisha yangu ya familia nzima”

“Okay kama ni India ni mji gani ambao utahitaji kuishi?”

“Mji ambao nina penda tukaishi ni Kozhikode”

“Mmmn ni mji gani huo mke wangu”

“Kumbe India hujaitembea ehee?”

“Sio sana ila ile nchi ni kubwa mno”

“Yaa ni nchi kubwa sana. Ila mji huu wa Kozhikode upo pembezoni kabisa mwa bahari na ni mji ambapo haun wau wengi ukilinganisha na miji mingi. Naamini pale tuna weza kununua ardhi kubwa tukajenga makazi yetu na mtoto wetu”

Nikautafuta mji huu katika mtandoa na nikauangalia ni mji ambao kweli hauna mambo mengi kama miji mingine.

“Kama umepapenda mke wangu sawa ngoja nimpe kazi Willy ya kuangalia nia maeneo gani ambayo yapo wazi na yana uzwa”

“Sawa mume wangu, ndio mana ana kupenda. Una nisikiliza”

“Nisipo kusikiliza wewe nimsikilize nani mke wangu.”

“Umeona ehee?”

“Ndio hivyo mke wangu, napenda wewe na mwanangu muishi maisha ya furaha”

“Nashukuru kusikia hivyo”

Nikampigia simu Willy na nikampa kazi ya kunitafutia eneo kubwa ambalo nita linunua kwa ajili ya makazi ya maisha yangu.

“Vipi lakini Judy ana endeleaje?”

“Namshukuru Mungu ana endelea vizuri, sasa hivi amelala, kidogo hii mimba ina mpa usingizi wa mara kwa mara”

“Hilo ni jambo la kawaida kwa mama mjamzito. Basi wewe ni tafutie hilo eneo nililo kuambia kisha utaniambia”

“Sawa kaka”

“Nikutakie usiku mwema”

“Nawe pia kaka”

“Hivi yule rafiki yenu Gody bado yupo na mpenzi wake?”

“Siku nyingi walisha achana”

“Weee”

“Ohooo Gody kawa mcharo”

“Hahahahaha wacha weee”

“Oooho tatizo lake lilisha isha hivyo ndugu yetu kawa mcharo. Full kubadilisha wadada”

“Jamani muambieni ata kufa”

“Ahaa ana lijua hilo ila ata tulia tu”

“Kweli muda wake ukifika ata tulia. Alafu mume wangu kwa nini tisiwashawishi Willy na Judy tukaenda kuishi nao huko?”

“Mmmm ngoja kwanza eneo hilo lipatikane”

“Sawa mume wangu, kwa maana hata Judy si ana weza kuachana na kazi”

“Yaa ana weza kuacha kazi”

“Basi nitampa kiasi chochote cha pesa ili mradi tukaishi nao huko”

“Ngoja tuta waalika chakula cha usiku na tuzungumze nao”

“Sawa mume wangu”

Tukazungumza mambo mengi na mke wangu ikiwemo mambo ambayo tutafanya tukiwa nchini India kwani ili maisha yetu yaendelee kuwa bora ni lazima kuingia kwenye biashara ambayo itatuingizia pesa za kutosha. Tukatazama filamu kadhaa hadi usingizi ukatupitia.

Siku ya mazishi ikawadia kuwazika wananchi walio fia kanisani. Nikiwa kama kiongozi wa nchi nikajumuika na wana ndugu pamoja na wananchi wengine katika mazishi ya pamoja ya wananchi hawa. Kusema kweli ni msiba mzito na umegusa hisia za wananchi wengi na wamejitokeza wa dini mbalimbali.

Muda wa mimi kuzungumza ukawadia, huku wananchi wengi wakisubiria nizungumze. Kala ya kusimama Cauther akanishika kiganja cha mkono wangu wa kulia ikiwa ni ishara ya kunipa ujasiri. Nikasimama eneo ambalo lina vipasa sauti huku nikitazaa majeneza mengi sana yaliyopo eneo hili.

“Bwana Yesu asifie”

“Amen”

Watu wote waliitikia.

“Tumsifu Yesu Kristo”

“Milele amen”

“Ndugu zangu wanachi, ni masikitiko makubwa ambayo sisi kama taifa tumepata. Ndugu zetu wakubwa na watoto wamelala kwenye haya masanduku, walitamani siku kama ya leo wawe pamoja nasi katika eneo jengine na sio eneo kama hili”

Nikanyamaza kimya huku nikitazama watu hawa wengi walio kusanyika.

“Kuzika watu mia tano na stini na mbili kwa wakati mmoja ni jambo ambalo lina tisha na kuogopesha. Ila kama nilivyo waahidi, serikali yangu au hata serikali inayo kuja kuchukua hapa nilipo ishia. Itahakikisha ili swala lina lipwa. Ita hakikisha hili swala lina kuwa ni swala la kihistoria na walio husika wata lipa.”

“Siku ya tukio nilifanikiwa kuingia ndani ya kanisa. Kwa kweli ilikuwa ina tisha na kuumiza. Popote aliye husika na hili tuta mshuhulikia. Vikosi vyetu vita washuhulikia kisawa sawa.”

“Tuzidi kuwaombe kwa mwenyezi Mungu aweze kuwapa mapumziko mema. Mungu azilaze mahali pema roho za Marehemu amen”

Baada ya kumaliza kuzungumza nikashuka katika eneo hili na niakrudi kwenye kiti changu. Miili yote ikazikwa kwa pamoja na wanajeshi. Baada ya mazishi kuisha nikarudi ikulu na mke wangu.

“Ila watu ni wengi sana mume wangu?”

“Watu miatano na kitu ni wengi sana”

“Ila kwa nini hao watu wana kosa roho ya imani jamani”

“Ahaa sijui kwa nini yule mzee amekuwa katili kiasi hicho”

“Ila malipo ni hapa hapa duniani”

“Kweli mke wangu”

Ruben akaingia nyumbani kwangu hapa.

“Ndio Ruben”

“Muheshimia raisi una simu ya kikazi”

“Sawa”

Nikanyanyuka katika sofa hili, nikambusu mke wangu katika lipsi zangu na tukatoka ndani hapa na Ruben.

“Imetoka wapi?”

“Marekani, raisi wa Marekani ana hitaji kuzungumza na wewe”

“Sawa”

Nikaingia ofisini kwangu na nikaa katika kiti changu na kupokea simu hii iliyo pigwa kwa video call.

“Habari za usiku muheshimiwa raisi”

“Salama, japo huku kwetu sasa hivi ni mchana”

“Oho ni kweli masaa yetu yamepisha”

“Ndio ndio.”

“Kwanza nitoe pole kwa msiba mkubwa ambao umeupata. Kwa kweli ni jambo la kuhuzunisha na tukumbuke sisi ndio nchi zenye nguvu kwa sasa duniani. Tuna uwezo wa kumsaka yoyote, kama Osama aliweza kuuwawa na mmoja wa wapelelezi wa nchi yako, Dany ina kuwaje huyu tushinwe kumuangamiza. Ina kuwaje tushindwe kuwaangamiza hawa Scorpion.”

Nikashusha pumzi huku nikimtazama raisi huyu wa Marekani.

“Una plan gani katika kuwakabili hawa watu?”

“Nahitaji tuisaidiane katika maswala ya kiusalama. Utoe timu ya vijana wako bora hata watano nami nitoe timu ya vijana wangu watano bora. Waungane kwa pamoja na waanzishe oparesheni ya siri. Itakayo hakikisha hichi kiosi kina sambaratishwa”

“Hivi una jua kwamba katika serikali yako Scorpion wapo?”

“Yangu?”

“Ndio yako. Nina kila aina ya details ya kikosi hicho. Hivyo hata washauri wako kadhaa nao wapo kwenye hicho kikundi hivyo ina bidi uwe makini. Safisha kwanza serikali yako kisha tuta rudi na kuzungumza.”

“Nakuahidi kufanya hilo na je una weza kunisaidia”

“Kukusaidia nini?”

“Hao wanao husika ni nani na nani?”

“Nchi yangu na yako zipo mbele sana kwenye teknolojia na upelelezi. Hakikisha una watambua wewe mwenyewe ili kama ni kuwachukulia hatua uwachukulie wewe mwenyewe. Nimebakisha siku thelathini na mbili kabla ya kukabidhi ofisi. Hivyo niwahi kabla sijaachia madaraka.”

“Nimekuelewa muheshimiwa raisi nitalifanyia kazi kwa umakini”

“Nashukuru kwa hilo”

Nikakata simu hii na nikajifikiria kwa muda, kisha nikanyanyua mkonga wa simu yangu. Nikaminya baadhi ya namba na nikampigia simu mshauri wangu ambaye kwa sasa tayari chama kilichopo madarakani kimesha mtangaza kama mgombea uraisi.

“Ndio muheshimiwa raisi”

“Nakuomba ofisini kwangu”

“Sawa”

Nikakata simu na baada ya dakika tano akaingia ndani hapa.

“Ndio muheshimiwa raisi”

“Naamini kwamba una tambua tuta fnaya juu chini hadi uwe raisi wa hii nchi”

“Ndio ndio”

“Kampeni zako zina anza kehso kutwa. Najutambua kwamba Scoprion wamemsimamisha mpizani wako na kumpa nguvu ili awe kiongozi wa hii nchi. Naamini huto niangusha”

“Siwezi kukuangusha muheshimiwa raisi. Nita hakikisha kwamba tuta chukua hichi kiti kwa namna zote.”

“Raisi wa Marekani nimetoka kuzungumza naye sasa hivi. Ana hitaji tuunde timu ya vijana watano kutoka Tanzania na watano kutoka Marekani wapambane na Scorpion ila nikamueleza jamano moja kwamba”

“Ehee”

“Ndani ya serikali yake kuna hao wana chama wa Scorpion hivyo itakuwa ni ngumu kwa sisi kupiga step yoyote kwenye hilo. Hivyo nimepatia kazi ya kuhakikishaa na watambua na kuwachukulia hatua kabla ya siku hizi thelathini kuisha. Au nimekosea kumuambia hivyo?”

“Hujakosea muheshimiwa raisi upo sahihi kabisa kwenye hilo na kama huto kuwepo madarakani nikuhakikishie kwamba nita lishuhulikia”

“Nashukuru sana mzee wangu. Kuwa raisi ni msalaba, yaani hapa nina elewa nini maana ya kuwa raisi. Naomba usiwe mtu wa kuyumbishwa. Simama kwenye msimamo wako na amani kile unacho kifanya kwamba ndio dira ya nchi”

“Nimekuelewa muheshimiwa na nimepa udhaifu wa mpinzani wetu”

“Udhaifu gani?”

Simu yangu ya mkononi ikaanza kuita. Nikaitoa mfukoni na kuona ni namba ya Willy.

“Samahani”

“Bila sahamani muheshimiwa”

Nikapokea simu hii na kuiweka sikioni mwangu.

“Ndio dogo”

“Kaka nina suprize na zawadi yako”

“Zawadi gani?”

“Upo karibu na ofisini kwako?”

“Ndio nipo ofisini”

“Washa computer yako”

“Ipo on”

“Kuna video nimekutumia kwenye email yako”

Nikaifungua email yangu na nikaona video hii. Nikaifungua video hii nikajikuta nikitoa macho ya mshangao mara baada ya kumuona makamu wa raisin a mke wa raisi aliye pitwa wakiwa katika fukwe ambayo pembeni yake ina jumba kubwa la kifahari na eneo hilo lina walinzi wengi sana wakiwalinda.

“Dogo hapa ni wapi?”

“Hiyo ni video ya Satelaite bwana, nimeichukua dakika tano zilizo pita na hapo wapo Zanzibar kwenye hiyo nyumba ambayo nilivyo ifwatilia nimeona ina milikiwa na bwana Leonard Leopard. Yeye ni Muingereza. Nimejariubu kuingia kwenye database ya kundi la Scorpion nimeona naye ni miongoni mwa wafanya biashara walipo hapa Tanzania nao pia ni wana chama wa Scorpion”

Nikajihisi joto kidogo mwilini mwangu. Nikavua kuti langu la suti huku nikimtazama mzee huyu kwa macho ya hasira sana.

“Kaka”

“Nakusikia”

“Niambie niwafanyaje kwa maana nina uwezo wa kutuma bomo likaenda kuwasambaratisha eneo hilo zima na hapa ninavyo zungumza satelaite imesha elekea kwao na hawajui kwamba nimeweza kuwanasa kwani eneo hilo lilikuwa halionekani kabisa kwenye satelaite wala ramani ya Tanzania”

Nikajikuta nikuna kichwa changu huku nikitafakari ni nini cha kumjibu Willy kwani huyu mshenzi ndio amehusika kwenye vifo vya watu mia tano na stini na mbili na sasa hivi amekaa na kustarehe kwenye nchi ambayo ardhi yake amesha imwagisha damu.




“Nahitaji hii kazi kuifanya peke yangu”

“Ngoja kwanza kaka. Una taka kuniuambia una taka ukamkamate wewe mwenyewe?”

“Haya yote anayo yafanya ni kutokana ana mimi kuwa madarakani. Hivyo nahitaji hili swala kulimaliza mimi mwenyewe”

“Mkuu una hisi kumuua yeye ina weza kusaidia kwa Scorpion kuto kuandama?”

“Una hisi nifanye nini. Muna hitaji nikae kimya na kuifumbata mikono yangu na kwenda kumuomba msamaha.”

“Sijamaanisha hivyo”

“Ila?”

“Muheshimiwa wewe ni raisi, una tegemewa na….”

“Wewe ndio raisi, una paswa kujua njia gani ya sisi kuhakikisha tuna mkamata yule mpuuzi. Kabla ya kukalia hichi kiti nilikuwa ni mpambanaji. Niliua kwa ajili ya hii nchi iwe salama. Hivyo nahitaji kulishushulikia hili mimi peke yangu”

Nilizungumza huku nikimtazama mshauri wangu usoni mwake.

“Nahitaji kuhakikisha kwamba huyu mpuuzi nina mua. Willy”

“Ndio kaka”

“Hakikisha kwamba una waangalia hawa wapuuzi na wasiondoke hili eneo umenielewa?”

“Sawa kaka”

Nikanyanyuka na kuanza kuelekea mlangoni”

“Mkuu una weza ukawa ni mtego”

Mshauri wangu alizungumza na nikajikuta nikisimama na taratibu nikageuka.

“Tafadhali, usiliendeshe hili swala kihasira. Naomba uliendeshe kwa kutumia akili na moyo wako. Sawa uta muua, je umefikiria kuhusiana na mke wako na mwano. Je una jua ni kitakacho wapata. Nipo hapa kwa ajili ya kukushauri kwa manufaa ya maisha yako ya sasa na maisha ya baadae ila kama huto jitaji kunisikia sawa. Ila ushauri wangu mimi ni huo.”

Japo ni jasiri na nina kuw ani mtu wa maamuzi ya haraka sana ila unapo nitajia mwanangu na mke wangu basi huwa una nimaliza nguvu sana kwa maan nilisha poteza ndugu zangu nilio kuwa nao toka utotoni, sasa ikitokea Cauther na mwanangu nao wakapotea kutokana na maamuzi yangu ya kijinga ina weza kunigarimu. Nikarudi kwenye kiti changu na nikakaa, nikaitaza video hii iliyopo katika computer yangu.

“Wewe sasa hivi ni baba. Una mambo mengi ya kuyafanya kwa ajili ya familia yako na mwanao. Naomba hili swala nilishuhulikie mimi mara baada ya kuchukua madaraka.”

“Hadi uchukue madaraka?”

“Ndio, tuna uchaguzi hapa mbele na zimebaki siku chache kabla sijaanza kampenzi zangu za uraisi. Endapo uta muua huyu mzee, hakutokuwa na usalama wowote katika uchaguzi. Yana weza kutokea yale ya ndugu zetu wa Kenya. Watu wakaua wenyewe kwa wenyewe kwa maana wana ushawishi na hawato ona hasara kuapandikiza watu wataakao fanya fujo kwenye kampeni na mwisho wa siku ichi ikaingia kwenye machafuko makubwa saidi ya haya yaliyo tusibu”

Nikashusha pumzi huku nikimtazama mshauri wangu usoni mwake.

“Nikiwa kama raisi nini nifanye?”

“Kwa sasa fanya kama hujui chochote, ila kutokana wamesha ingia Tanzania, utakacho kifanya ni sisi kufwatilia nyendo zao taratibu na tuta wabana, Ngoja nichukue madaraka, nita wanyoosha. Sasa hivi wewe bado kijana na hata miaka arobaini hujafikisha. Una ndoto kubwa na na mambo mengi sana ambayo una paswa kuyafanya kwa sasa hivi niachie hili swala rasmi nilishuhulikie”

Nikajifikiria kwa muda kidogo.

“Nakuomba mkuu niache nilishuhulikie hii”

“Sawa naomba nikapumzike”

“Hakuna shaka na kuna jambo moja mkuu ina bidi utusaidie kama chama”

“Jambo gani”

“Kwenye ufunguzi wa kampeni yetu ya kwanza. Ina bidi uweze kuhudhuria ili kunitambulisha kwa wananchi nan na kama unavyo fahamu una ushawishi mkubwa sana kwa watu hivyo una weza kunisaidia kwenye hili”

“Hakuna shaka si kesho kutwa?”

“Ndio”

“Hakuna tatizo”

“Nashukuru mkuu”

Nikanyanyuka na kutoka ofisini hapa. Moja kwa moja nikaelekea ninapo ishi.

“Vipi kazi imekwisha mume wangu?”

“Yaa nilikuwa nina zungumza na raisi wa Marekani. Mke wangu kuna jambo naomba unishauri”

“Jambo gani?”

“Tumegundua makamu wa raisi yupo hapa nchini Tanzania”

“Nini?”

“Ndio na wapo Zanzibar kwenye fukwe moja. Yupo na mke wa raisi aliye toka madarakani wana endelea kula maisha”

“Mungu wangu, sasa mume wangu si mukamkamte?

“Hilo jambo nilikuwa nalo kichwani na nilitaka kwenda kuifanya hiyo shuhuli mimi mwenyewe ila nikashauriwa na mashauri wnagu kuachana na hilo jambo”

“Kwa nini mume wangu?”

“Kwa sababu yaw ewe na mtoto wetu. Mimi nina weza kuwalinda sawa ila nina hofia kufanya makossa ya kuwapoteza kama nilivyo wapoteza ndugu zangu”

Mmmm hilo nalo neon mume wnagu”

“Yaa nakupenda mke wangu, bado tuna safari kubwa na ndefu sana kwneye maisha yetu hivyo kwa sasa sihitaji kufanya kosa jengine la kukupoteza wewe na mwangu”

“Hilo nalo ni neon mume wangu. Kama ume amua kuachana nao naomba uamue kutoka moyoni mwako. Usiwafwatilie kabisa”

“Sawa mke wangu nimekuelewa”

Siku ya ufunguzi wa kampeni za chama kilichpo madarakani ukawadia. Wananchi wengi wakajitokea katika viwanja vya jagwani. Huku nami nikiudhuria katika mkutano huu mkubwa ili mmdani mgombe ampya wa raisi. Shangwe na nderemo zikaendelea huku ikwia hii ndio mara yangu ya kwanza kwa mimi kuhudhuria katika katika mkutano kama huu wa kiasa kwani kwenye maisha yangu yote sikuwahi kuhudhuria siku hata moja. Baada ya shamra shamra zote za wana siasa hawa wambao maneno yao mengi ni matamu kama asali ila ukirudi upate wa utekelezaji hakuna kitu kabisa. Ukawadia muda wangu wa kusimama mbele ya wananchi hawa. Nikawasalimia kwa furaha na shangwe ikatawala huku wengi wao wkainishangilia kwa kuniita raisin a wana matarajio makubwa nami niwe raisi.

“Naombeni tusikilizane ndugu zangu”

Nilizungumza ili kuzuia shangwe hizi zinazo endelea.

“Nashukuru sana ndugu zangu kwa kuja. Wingi wenu una dhihirisha kabisa kwamba tumesha shida uchaguzi au sio”

Wananchi wote wakashangiliwa kwa furaha.

“Mimi sina mengi ya kuongea, nipende kumshukuru kwanza mwenyezi Mungu kwa kuniwezesha kunipa pumzi ya kuendelea kuishi hadi wakati huu. Niwashukuru ninyi pia kwa kunisaidia kuhakikisha kwamba ninaiongoza nchi kwa kipindi cha miezi mitatu. Ilikuwa ni mieszi migumu sana kwenye kazi yangu ambayo ilikuwa ni ngeni sana ila Mungu alinipigania kuhakikisha kwamba hadi leo nchi imefikia hapa”

“Nina imani wengi wenu muna tambu katiba ya nchi yetu ni nini ina hitaji. Katiba ya nchi yetu ina hitaji raisi awe na umri zaidi ya miaka arobaini na kitu. Mimi sijafikisha huo umri kwa sasa nina waletea chuma, mtu ambaye atahakikisha kwamba nchi ina kuwa salama na imara. Namleta kwenu, muheshimiwa Leonard Simba”

Wananchi wakashangilia na mshayri wangu akasimama katika kiti alicho kuwa amekalia na akanifwata sehemu nilipo simama. Akasalimiana na wananchi.

“Naombeni ndugu zangu popote mulipo mumpatie kura bwana Leonard Simba. Karibu muheshimiwa”

Mshauri wangu mkuu akaanza kuzungumza na wananchi walio jitokea eneo hili. Akatoa vipaumbele vyake katika pale atakapo ingia madarakani.

Wananachi wakafurahishwa na vipaumbele hivyo kwani moja kwa moja vina gusa ulinzi wa wananchi, nchi pamoja na kuwaendeleza kiuchumi.

Baada ya mkutano huu kuisha nikarudi ikulu.

“Kuwa mwana siasa ni kazi sana”

“Kwa nini mume wangu?”

“Ahaa kuongea mbele za watu na kuzungumza vitu ambavyo huna uhakikka kama una weza kuvikamilisha sio jambo dogo mke wangu”

“Yaani kazi kweli. Ila ndivyo wananchi wana penda. Hivi una hisi kwamba ukiwaambaiw ananchi kwamba sito weza kuwakamilishia haja zao una hisi wata kuchagua”

“Hahaha hawawezi labda uchaguliwe na mke wako na familia yako”

“Hahahaaa”

“Ila namshukuru Mungu mambo yana kwenda kufika ukingoni”

“Hata mimi mume wangu nimechoka sana kukaa hapa ikulu”

“Usijali mungu ata tusaidia tuta ondoka na ina bidi tukisha kabidhi madaraka. Tukae Tanzania kwa wiki kadhaa tukiwaaga ndugu zetu kisha ndio tuondoke”

“Hakuna shaka mume wangu.”

“Umefwatilia ununuzi wa lile eneo?”

Nilimuuliza Cauther kwani tayari tumesha pata eneo nchini India katika mji ambao tuna uhitaji na ndipo makazi yangu mke wangu yatakapo kuwa.

“Ndio mume wangu, leo nimemualika chakual cha usiku balozi wa India hapa nchini Tanzania ata kuja saa mbili hii”

“Ahaa sasa saw make wangu, nashukuru kwa juhudi zako”

“Usijali mume wangu ni moja ya majukumu yangu”

“Asante”

Majira ya saa mbili balozi wa India nchini hapa Tanzania ambate ni mwana mama akafika ikulu, na tukajumuka naye kwenye chakula cha usiku.

“Chakula chako mrs Eddy ni kitamu sana”

“Nina shukuru sana kwa kukipenda”

“Huwa napendelea sana vyakula vya asili vya nchi hii ya Tanzania”

“Hivi kwa India hivi vyakula vina patikana?”

“Hapana labda sehemu chache sana, ila kwa ujuzi wangu sujawahi kuviona”

“Mume wnagu kwa nini tusifungue mgahawa mkubwa tukiwa nchini India na tukapika vyakula hivi?”

“Ni wazo zuri mke wnagu nani ata kuwa mpishi?”

“Mimi na wewe”

“Hahaaa hilo nalo ni wazo zuri sana jamani”

Mwana mama huyu alizungumza kwa furaha.

“Muna jua mutakuwa ni kivutio kikubwa sana kwa watu pale watakapo jua aliyekuwa raisi wa nchi yenye nguvu duaniani yeye na mke wake wana mgahawa mkubwa India na wao ndio wapishi”

“Umeona mama Sharma”

“Yaa ni jambo na wazo zuri sana.”

“Naamini mke wangu ata lisimamia hilo ina bidi mke wangu uniazishie masomo ya kujifunza kupika”

“Hahaaa wala usijali mume wangu. Hapa mapishi yametulia.”

“Kusema kweli nina penda sna couple yenu. Yaani ina vutia kweli kweli”

“Tuna shukuru sana”

“Lile eneo nilizungumza na raisin a nikamuonyehsa picha za eneo mululo liomba na nikamueleza kwamba una mpango wa kwenda kuishi kule. Kusema kweli amefurahi sana ten asana”

“Tunashukuru kwa hili”

“Na pia amesema eneo hilo ataemua kuwapatia bure kabisa na nimetumiwa hati miliki ya eneo hilo na kilicho salia ni nyingi kutia saini, nami nimesha tia saini”

Balozi akatukabidhi bahasha nikaitoa karatasi zilizopo ndani ya hii bahasha. Nikazisoma na kujikuta nikitabasamu, nikamkabidhi mke wangu naye akazisoma karatasi hizi zinazo onyesha umilkiki wa kukabidhiwa eneo hilo.

“Tunashukuru sana muheshimiwa balozi.”

“Tuna wakaribisha sana India, sisi na nyinyi ni kama ndugu kabisa. Pia raisi ana omba muzungumze naye”

“Sawa una weza ukampigia simu”

Balozi akampigia simu raisi wa India na baada ya muda simu ikapokelewa.

“Muheshimiwa raisi habari ya muda huu”

“Salama kabisa habari za Tanzania”

“Mungu ana bariki. Nipo na raisi wa Tanzania hapa pamoja na mke wake”

“Ohoo nafurahi sana kusikia hivyo”

“Wana hitaji kuzungumza na wewe”

“Wapatie simu niongee nao”

Nikakabidhiwa simu hii na Cauther akasogea karibu yangu na sote tukaoneka kwenye kioo cha simu hii kwani mawasiliano haya ni ya video call.

“Habari muheshimiwa raisi”

“Salama bwana Eddy. Nina shukuru na kufurahi kusikia kwamba ukimaliza muda wako uta kuja kuishi nchini kwangu India”

“Nami nashukuru kwa kwlei na nina sema asante mimi na mke wangu kwa kutupatia eneo ambalo nitakuwa ni nia ishi”

“Asante sana kwa kulipokea”

“Huhu ni mke wangu ana itwa Cuther”

“Nashukuru kukufahamu bi Cauther”

“Nashukuru sana”

“Muheshimiwa raisi Eddy siku ukija India nina omba sana mufike ikulu na niwapokee”

“Nashukuru sana muheshimiwa na nita fanya hivyo”

“Niwatakie muda mwema na karibu sana India”

“Asante nawe pia”

Nikamrudishia balozi simu akamaliza kuzungumza na raisi wake na tukaendelea kupata chakula cha hichi cha usiku. Mara baada ya chakula tukatia sahihi kwenye hati hizi za umiliki wa eneo tulilo pewa na serikali ya India.

Balozi akaondoka ikulu hapa na ikwa ni moja ya furaha kwetu kwani tulisha andaa kiasi kikubwa sana cha pesa.

“Ina bidi mke wangu uanze kuchagua nyumba ambayo tuta jenga eneo hili”

“Sawa mume wangu hakuna shaka”

“Kuwa na wewe baraka zina funguka tu”

“Kweli mume wangu?”

“Ndio mke wangu”

“Asante mume wangu, ndio maana nina kupenda sana”

“Nina kupenda pia mke wangu”

Simu yangu ikaanza kuita, nikaitoa mfukoni na kuona private namba ambayo oja kwa moja nihna jua anaye nipigia ni makamu wa raisi. Nikaipokea na kuiweka simu sikioni.

“Eddy Eddy”

“Una hitaji nini?”

“Hata salamau kijana wangu”

“Nenda kwenye pointi una hitaji nini?”

“Nahitaji kuzungumza mimi na wewe kama wanaume. Nahitaji tuongee kiumne mimi na wewe. Tusiishie maisha ya kukimbiana kimbiana”

“Wapi na lini?”

“Leo saa sita usiku, nipo katika nyumba ambayo nilikukamata ulipo kuwa kibaka mdo mdogo hivyo nahitaji tuonane na njoo peke yako kwa manaa endapo uta kuja na mtu mwengie chochote basi kina weza kutokea. Naamini ume nielewa”

Nikashusha pumzi huku nikimtazama Cauther usoni mwake kwani kuitwa kwangu huku sijui mzee huyu ana moango gani na mimi na kutokana nina jiamini. Ni lazima nihakikishe nina onana naye vyovyote ilivyo lazima ajibu yale yote nitakayo muulia na endapo ata shindwa basi na yeye kwa upande wake chochote kina weza kutokea.



“Ndio”

“Saa sita usiku”

Makamu wa raisi akakata simu. Nikashusha pumzi huku Cauther akinitazama.

“Kuna nini mume wangu?”

“Kuna sehemu nahitaji kwenda saa sita usiku kuna maswala yakiserikali nataka nikayashuhulikie”

“Sawa mume wangu uwe makini tu. Tambua nina kupenda na mwanao pia ana kupenda na wewe ndio tegemeo letu”

“Usijali mke wangu. Ngoja nizungumze na walinzi wangu”

“Sawa baby”

Nikambusu Cauther katika paji lake la uso na nikatoka ndani hapa.

“Ruben njoo ofisini kwangu”

“Sawa mkuu”

Tukaongozaa hadi ofisini kwangu.

“Nahitaji kutoka iluku muda huu na kuelekea Bagamoyo. Nahitaji nitoke mimi na wewe tu na sihitaji mtu mwengine atambue”

“Sawa muheshimiwa raisi ni matembezi binafsi au?”

“Kuna swala binafsi nina kwenda kulishuhulikia”

“Sawa muheshimiwa ngoja niandae mazingira”

“Poa poa”

Ruben akatoka ndani hapa na baada ya dakika kumi akarudi.

“Tayari muheshimiwa nimesha andaa mazingira.”

“Sawa”

Tukatoka ndani hapa na moja kwa moja tukaongoza na kupita njia za siri zilizipo chini ya ardhi hadi tukatoka nje ya ikulu na kukuta gari alilo liandaa Ruben.

“Naomba funguo. Naendesha”

Ruben akanikabidhi funguo tukaingia ndani ya gari na kuondoka eneo hili.

“Una weza kuwa msiri?”

“Ndio muheshimiwa raisi ndio kazi yangu”

“Makamu wa raisi amenipigia simu leo hii anahitaji kukutana na mimi”

“Huyu gaidi?”

“Ndio”

“Muheshimiwa ndio una taka twende sisi wawili peke yetu?”

“Nina kwenda peke yangu”

“Muheshimiwa ina bidi kutoa ripoti kwa vyombo vya usalama. Yule ni gaidi ana weza kukuua mkuu”

“Nisikilize Ruben. Mimi sio rahisi kuuwawa kama unavyo fikiria. Hivyo usi panic na usimueleze mtu wa aina yoyote kwenye hili”

“Mkuu, una nipa wasiwasi?”

“Usiwe na shaka. Wewe tulia”

Nikamsihi sana Ruben kuto kuwa na wasiwasi kwa maana endapo lolote baya litanipata basi yeye ata wajibishwa na jamuhuri ya Muungano wa Tanzania. Ruben akakubali na nikafika katika nyumba yangu ya siri iliyopo Bagamoyo.

“Ndio hapa munapo onana?”

“Hapana hii ni nyumba yangu, kipindi nipo kitengo cha X tulikuwa tuna itumia kama eneo la kukutana, kupanga mipango na kuhifadhi silaha zetu za siri”

“Ahaaa sawa sawa”

Tukashuka ndani ya gari na tukaingia ndani. Nikawasha taa, tukakaribishwa na vumbi jingi lililomo ndnai humu kwa maana hakuna anaye ingia wala kufanya usafi ndani ya nyumba hii. Ruben akashangaa picha za wezangu wa kikundi cha X zikiwa ukutani.

“Huyu ni wewe mkuu?”

“Yaa kipindi hicho bado mdogo mdogo. Hapo nina miaka ishirini na mbili kitu kama hicho”

“Aisee kweli hapa ukuwa na sura ya kitoto sana”

“Yaa hawa wezangu wamesha tangulia mbele za haki kwa sababu ya uovu wa makamu wa raisi”

Nilizungumza kwa suti ya uchungu huku nikifuta vumbi katika vioo vya picha hizi. T

“Njoo huku”

Tukaingia katika chumba kilichopo ardhini ambacho watu wa pekee nilio waleta humu ni Willy, Judy na Cauther.

“Katika chumba hichi kuna kila aina ya silaha ambayo wewe una ijua”

“Waooo”

“Naona muna mikanda ya Kung Fu”

“Ndio tumefuzu kwa level ya juu sote wanne. Pia ni manija”

“Weee mkuu kumbe wewe ni mtu hatari sana?”

“Hadi leo haujajua kama nimi ni mtu hatari?”

“Nilijua mkuu ila sikujua ni kwa upana gani. Ila nilishuhudia ile siku pala Israel, kimoyo moyo nilikuwa nina jisiema kwamba mlinzi badala ya kumlinda raisi, yeye ndio ana lindwa”

“Laiti kama ningekuacha upambane unge uwawa na wewe”

Nikafungua moja ya kabati ambalo lina nguo zangu za kininja pamoja na vifaa vyake.

“Waoooo!!”

Ruben alishangaa.

“Hivi wewe umepitia mafunzo gani?”

“Ni ukomandoo pekee mkuu”

“Katika kikosi kipya cha X kitakacho undwa omba na wewe uingine na upate mafunzo kama haya. Ukiwa ninja ina manaa una weza kuua watu mia moja ukiwa peke yako”

“Mia!!?”

“Ndio”

“Kwa bunduki au?”

“Sio bunduki, kwa upanga”

“Upanga”

“Ndio”

“Mmmmmm, ina kuwaje kuwaje mkuu?”

“Maninja halisia huwa wana mbinu fulani ambazo tuna zihusisha na imani za kishirikina. Ninja ana uwezo wa kupotea dakika yoyote mbele ya mtu pale atajapo zungumza maneno fulani”

“Mmmm mkuu samahani. Hayo mambo si ya filamu tu za kichina na wajapani”

“Una taka kuona tunavyo fanya?”

“Kama huto jali mkuu”

Nikatabasamu huku nikimtazama Ruben usoni mwake. Nikavua nguo zangu hizi za kawaida na nikavaa nguo hizi za kichini. Na huwa nikivaa nguo hizi huwa kuna hali fulani nina ihisi katika mwili wangu ambayo ni tofauti kabisa na hali ya kibinadamu.

“Upo tayari?”

“Ndio mkuu”

“Huto kimbia?”

“Hapana mkuu”

“Toa bastola yako”

“Eehee?”

“Toa bastola yako”

Ruben akachomoa bastola yake kiunino mwake.

“Nilenge”

“Mkuu!!”

“Nilenge na unipige risasi”

“Mkuu….ni”

“Pia risasi”

Nikamfokea Ruben na akajikuta akifyatua risasi bila ya kupenda. Nikapotea mbele yake na kumfanya astuke, nikasimama nyuma yake.

“Mkuu”

Ruben alizungumza huku akibabaika.

“Nipo nyuma yako”

Akageuka na kujikuta akistuka na bastola ika muanguka chini.

“Una ogopa mbona wakati nilikuambia usiogope”

“Mkuu sijawahi ona kitu kama hichi”

“Kwenye movie si umeona”

“Nilihisi ni oongo”

“Sio uongo. Kuna vitu vya uongo na vitu vya uhalisia, acha kuhema sana kuna kazi ya kufanya mbele yako”S

Ruben akavuta pumzi nyingi kisha akaziachia taratibu.

“Hili ulilo liona usimuambie mtu yoyote”

“Sawa mkuu”

“Tuondoke”

“Unaondoka na mavazi haya?

“Ndio beba haya mavazi yangu”

“Ruben akabeba mavazi yangu haya nakabeba silaha zangu za kininja. Tukaingia ndani ya gari na kuondoka eneo hili huku safari hii Ruben akiwa ndio dereva. Nikamuekeza hadi nyumbani kwa makamu wa raisi. Tukasimama eneo la mbali kidogo. Nikatazama saa iliyopo katika gari hili na zimebaki dakika tano kabla ya kufika saa sita usiku.

“Kaa hapa na unisubirie”

“Sawa mkuu”

Nikashuka ndani ya gari na nikaanza kukimbia kwa kasi hadi ilipo nyumba ya makamu wa raisi. Nikaruka ukuta huu mrefu na nikatua ndani ya nyuma hii kimya kimya. Ulinzi ulipo nyumbani hapa sio wa kawaida, nikaingia hadi eneo la mein switch, nikazima umeme wa nyumba nzima, kisha nikaingia sebleni na ninakaka katika moja ya sofa ambalo lina tazama na makamu wa raisi ambaye yeye na walinzi wake bado wana shangaa sangaa.

“Ila kwa jirani upo”

Mlinzi mmoja alizungumza huku akifungua dirisha.

“Hembu angalieni kwenye socket”

Taa za nyumba nzima zikawashwa na watu wote wakashangaa kuniona ndani hapa huku mkononi mwangu nikiwa nimeshika silaha zilio kaa muundo nyota ambazo enendapo nina mrushia mtu na ikamchoma mwilini mwake ana kufa haraka kwani ina sumu kali.

“Wewe ni nani?”

Makamu wa raisi aliniuliza huku walinzi wake wakiwa wameninyooshea bastola zao. Nikavua kitambaa kilicho funika kichwa changu chote na kuacha macho pekee. Wakazidi kushangaa.

“Waambie wapuuzi wako waweke silaha zao chini”

Makamu wa raisi akatoa ishara kwa watu wake na wakaweka silaha zao chini.

“Naona umeamua kunijia kininja ninja?”

“Nenda kwenye mada iliyo kufanya unite hapa”

“Naombeni mutupishe”

Walinzi wake wote wakatoka nje ya seble hii na nikabaki mimi nay eye.

“Una tumia kinywaji gani?”

“Situmii kinywaji”

“Ohoo samahani”

Makamu wa raisi akafungua chup ya wyne akamimina kiasi kidogo katika glasi yake kish akairudisha chupa hiyo katika kabati na akarudi alipo kuwa amekaa.

“Una jua malengo yangu mimi ni nini”

“Sijawahi kujua malengo yako hivyo niambie kwa nini umeniiita na kwa nini umerudi Tanzania”

“Nimerudi Tanzania ili niwe raisi”

“Una wendawazimu. Una hisi kuna mtu yoyote ana weza kukupa nafasi ya wewe kuwa raisi?”

“Wewe ndio una nguvu ya kuwashawishi watu kunipa mimi kura”

“Nisikilize sijakuja kusiliza upumbavu wako”

Makamu wa raisi akatabasamu huku akinitazama kwa kejeli.

“Hivi una jua bila ya mimi kukufwata ile siku pale hotelini hadi leo ungekuwa ni dereva taksi wewe”

“Bora ningekuwa dereva taksi kuliko kuwa raisi kwa mana ningeishi kwa maani pasipo kubeba majukumu ambayo ni mazito kuliko mimi mwenyewe”

“Nilijua ni lazima yatakuwa ni magumu. Ndio maana nimehitaji kuja kuyachukua majukumu hayo. Ni kwa miaka zaidi ya arobaini nimekuwa nikiishi kwneye ndoto ya kuwa raisi. Nikawatengeneza wewe na wezako pamoja na wengine kwa ajili ya kunisaidia kufika malengo ila kwa bahati mbaya wewe ndio uliye salia”

“Kwa hiyo?”

“Nahitaji uniachie uraisi wangu.”

Nikatabasamu huku nikimtazama makamu wa raisi.

“Damu za watu ulio waua hazito kuruhusu uweze kuingia kwenye hichi kiti”

“Niambie una hitaji nini ili unipatie hiyo nafasi kwa maana yule mzee uliye muweka namuonea huruma kwani hato maliza hata siku mbili akiwa madarakani. Nitamua”

“Hivi unajiamini nini, kipi kinacho kufanya uwe jeuri kiasi hicho?”

Makamu wa raisi akakunja nne huku akinitazama machoni mwangu.

“Njoo”

Alizungumza kwa sauti ya juu. Mlango wa chumba kimoja ukafunguliwa na akatoka mwana mama ambaye ana fanan sana na mimi, yaani katika kumuangalia tu nikaiona sura yangu kabisa usoni mwake. Mwana mama huyu akaka kwenye sofa moja huku akinitazama kwa uso ulio jaa tabasamu.

“Naamini kwenye familia yako ukimuongeza mama yako basi utakuwa umepata family iliyo bora.

Makamu wa raisi alizungumza huku nikiendelea kumtazama mwana mama huyu.

“Eddy mwanangu”

Mwana mama huyu aliita huku machozi yakimlenga lenga machoni mwake. Akataka kumyanyuka nikamzuia kwa kumpa ishara ya kukaa alipo kwa maana huyu mzee simuamini na hawa watu wake anao jaribu kuwatengeneza wana weza kuwa hatari sana kwangu.

“Eddy mimi ni mama yako. Najua ni mengi niliyo kufanyia, ila nakuomba sana mwanangu unisamehe”

Mwanamama huyu alizungumza huku akipiga magoti chni na machozi yanamwagika usoni mwake. Nikamtazama makamu wa raisi kisha taratibu nikanyanyuka na nikachomoa upanga wangu ngongoni na kwa kasi ya ajanu nikauweka shingoni mwa mwana mama huyu na kumfanya macho yamtoke na kuanza kumtetemeka kwa woga.



“Wewe ni nani?”

Nilimuuliza mama huyu kwa sauti nzito na kumfanya azidi kutetemeka kwa woga.

“Weee ni nani?”

Nilirudia swali langu kwa lugha ya ukali na kumfanya mwana mama huyu kutokwa machozi.

“Weka upanga wako chini?”

Nilisikia sauti ya ukali nyuma yangu na kunifanya nimtazame makamu wa raisi ambaye macho yamemtoka kwa mshangao.

“Sijakuja kumuua mtu wa aia yoyote. Waambie panya wako watoke humu ndani?”

“Makamu wa raisi akampa ishara ya mlizi wake huyo kutoka dai hapa kwai ana nijua vizuri huwa sizungumzi mara mbili.

“Una weza ukawa na mtoto kama mimi?”

Niliendelea kumuuliza mwana mama huyu huku nikimkazia macho yake.

“Mtoto ambaye ulimuacha kwenye baridi kali na kumfunga funag kwenye Rambo na kumtupa mtaroni. Una weza kuwa na mtoto kama mimi eheee?”

Nilizungumza kwa sauti ya ukali huku upanga wangu ukiwa bado upo kwenye shngo ya mwana mama huyu.

“Mama sina na mama yangu alisha fariki hivyo siwezi kukukaribisha kwenye maisha yangu. Simama na uondoke. Moja, mbili…….”

Hata kabla sijamalizia kuhesabu mwana mama huyyu akakimbilia alipo tokea. Nikamtazama makamu wa raisi ambaye amejawa na woga mwingi.

“Kwa nini uliwaua wale watu kanisani?”

Jicho likamtoka makamu wa raisi.

“Eddy…..ila….hilo sio nililo kuitia”

Walinzi kama watano wakaingia kwa mpigo ndani hapa huku wakiwa wameshika bastola zaa na kunielekezea mimi.

“Wamekuja kufa si ndio?”

“Kabla hujafanya jambo lolote la kijinga fikiria familia yako. Mke wako mrembo na mwanao mzuri, wafikirie hao kisha ndio ufanye kitu cha kipuuzi”

Makamu wa raisi alizungumza kwa kujiamini akiamini kwamba huo ndio udhaifu wangu.

“Uta niua mimi, ila kuna watu nje wana wata waangamiza familia yako. Una weza kuwalinda ila huwezi jua ni nani ata waua kwani itakuwa ni hatari sana kwako”

Makamu wa raisi alizungumza kwa kujiamini huku akinitazama usoni mwangu. Nikashusha pumzi nyingi huku nikimtazama makamu wa raisi.

“Eddy mimi nidio niliye kuunda wewe. Mimi ndio niliye kufanya leo hii una onekana mtu kati ya watu. Chukualia kama mimi nisinge wasaidi wewe na wezako mungekuwa wapi sasa hivi?”

Makamu wa raisi alizungumza huku akinisogelea.

“Raisi wangekuwa wamesha wau na kuwaangamiza kwa wizi wenu. Au ningeamua kuwaua ule usiku ni nani ambaye angeuliza na kujali. Ila niliwaacha hao jna nikawalea kama wanangu, hususani wewe ndio nikupenda kuliko wezako. Na kama ningehitaji kukuua ninge kuua siku ambayo umekuwa dereva taksi, una hisi kwenye chama cha Scorpion hawajui kama upo hai?”

Makamu wa raisi akasimama hatua moja kutoka sehemu nilipo simama.

“Nipe ninacho kihitaji, niliunda Scorpion kwa lengo moja zuri. Kuifanya Tanzania kuzitawala nchi zote zilizopo duniani ila wewe unaichukulia ni kama maadui.”

“Kuua watu na kuwaangamiza kwa kuwalipua kwa mabomu na kuwaua kwa sumu hiyo ndio kuifanya iwe nchi tawala kwa kuua watu wako mwenyewe?”

“Eddy sio kila kifo au tukio linalo tokea ni kwa sababu ya bahati mbaya. Tuna ua kwa sababu, tuahitaji tazanina kuwa sehemu salama, ila kuna idadi ya watu lazima ipuguzwe. Hili ni kama machezo wa drafti, ili ushinde ni lazima ule kete za mpinzani wako na kuzipunguza ndio uta fanikiwa kuingia king na kushinda.”

Nikashusha pumzi nyingi huku nikimtazama makamu wa raisi.

“Eddy nina nguvu niliyo itengeneza kwa miaka yangu yote kuhakikisha kwamba siku moja nina kuja kufanikiwa. Tafadhali niachie uraisi, niachie nafasi hii, nahitaji kutimiza malemgo yangu”

Makamu wa raisi alizungumza huku akinitazama usoni mwangu

“Mshauri wako ni mtuw angu wa karibu sana. Sihitaji kumuu akiwa madarakani na kuifanya nchi iingie tena kwenye kipindi cha miezi mitatu ili atafutwe raisi wa muda.

“So hilo dio mumepanga kulifanya juu yake?”

“Ndio, sikufichi Eddy, nitakuamia ukweli kwa maana nina kujua wewe kuanzia ulivyo kuwa huna kitu hadi hapa ulipo. Tafadhali una nafasi hiyo kabla ya kampeni hazijaanza kuchachamaa”

Taratibu nikajikuta nikikaa katika sofa huku nikimtazama makamu wa raisi.

“Mimi sijawahi kuwa na mtoto, ila wewe una mtoto. Binti mzuri, binti atakaye kuwa na ndoto za maisha mazuri. Najua uan kwenda kuishi India, nenda kaishi huko na familia yako. Nina kuhakikishia kwamba uta kuwa salama. Hakuna atakaye kuigilia, hili la uogozi niachie mimi”

Makamu wa raisi alizungumza huku akiwa amechuchumaa mbele yangu.

“Jina lako lita kumbukwa kwenye hii nchi kama raisi wa kwaza mwenye umri mdogo na raisi ambaye alidumu kwa kipindi kifupi sana kwenye hii nchi. Nahitaji ndoto zangu kutimia kabla sijakufa, Eddy sitaki kumwaga damu tena, sihitaji kuua tena. Sihitaji kuendelea kuwaangamiza watu ili kuishinikiza serikali iliyopo madarakani kung’atuka.”

Nikamtazama makamu wa raisi usoni mwake.

“Mimi ndio ndio nilikuweka katika system hii. Mimi ndio niliye kuunganisha na viongozi wa juu na kuwa mtu wa kuaminika. Niache nigombanie uraisi kwa amani”

“Wananchi hawato kuamini?”

“Hilo niachie mimi”

“Una hisi uta weza kupita ikiwa una kashfa ya kuwa gaidi?”

“Eddy ni nani mwenye ushahidi kweye hilo? Kama hakuna mwenye ushahidi basi hakuna anaye weza kunizuia”

“Najua ulijua nipo Tanzania, una hisi mimi ni mjinga kulifanya eneo nililo kuwepo lionekane katika satelaite. Ila ulivyo kuwa kimya nikaona ni vyema nikuite na tuzungumze kama wana ume. Tuzungumze kama watu wenye lengo moja japo njia ni tofauti”

Nikamtazama makamu wa raisi.

“Sikutishi Eddy, ila ukweli ni huo, una weza kunia hata sasa hivi, ila tambua familia yako na wewe hawawezi kuwa salama. Uta shuhudia mke wako akipigwa risasi za kichwa mbele yako. Uta shuhudia mwanao akilawitiwa mbele yako. Hap outa kuwa huna uwezo wa kupambana. Uta umia, uta teska na uta lia kwa uchungu, Muda wako ni sasa kufanya mamuzi. Acha nigombanie uraisi uishi kwa amani”

“Fikiria kwanza familia yako kwani ndio muhimu kuliko nchi. Nchi hii ipo waliluwepo mashujaa wengi, wakafa na yamebaki majina yao na hakuna walicho nufaika. Ila ipo familia yako, hiyo ndio nafasi yako na hiyo ndio roho yaka. Fikiria hilo”

Nikaa kimya huku nikimtazama makamu wa raisi usoni mwake. Nikajifikiria kwa dakika tano kisha nikasimama.

“Uta kuwa raisi, ila endapo mke wangu, mwanangu au mashemeji zangu na wakwe wakipata tatizo lolote nikachugunza na nikajua ni wewe, jua kwamba nita kuaa kabla hata ya muda wako wa kuwa raisi haujaisha. Sinto ogopa kupoteza watu wangu, nita hakikisha kwamba una jua nini maaa ya nguvu ya Mungu iliyopo ndani mwangu, ndio mana alijaribu kuniua zaidi ya mara nne ukashindwa. Na kumbuka huwezi kuniua, ila mimi nina weza kukuua. Hivyo chunga sana”

“Nme kuelewa Eddy”

Nikapiga hatua hadi alipo simama makamu wa raisi.

“Mkono wangu huu, ume ua watu zaidi ya elfu moja na zaidi. Sijui ni roho ngapi zina niombea mabaya ila niliziua. Hivyo sishindwi kukuua wewe endapo uta vuka mstari”

Niluzungumza kwa sauti ya msisitizo.

“Umenielewa?”

“Ndio”

“Una jengine?”

“Huyu ni mama yako”

“Sina mama na usikae ukazungumza nina mama na usijaribu kutafuta kama nina mama. Umenielewa?”

“Ndio”

Nikapiga nikavaa kitambaa kinacho funika kichwa changu na kubakisha macho.

“Una mtoa vipi mgombea uraisi wa sasa?”

“Nitajua nini cha kufanya?”

“Uta mdhuru?”

“Hapana”

“Endapo uta mdhuru huto kuja kuwa raisi”

“Siwezi kufanya hivyo dili”

“Dili”

(Karibu nikuunge kwenye group la hadithi ya AIISSII u kill me chapter four. WhatsApp 0657072588. Ada ni 4000 kwa mwezi. Karibu sana)

Nikamtazmaa makamu wa raisi pamoja na walinzi wake. Nikazungumza maneno ambayo ukiwa ninja na katika mavazi haya una weza kupotea. Nikapotea mbele yao na nikatoea nyuma ya mmoja wao na kumuwekea kisu upanga huu shingoni mwake na kuwafanya wote wastuke.

“Naamini sasa umejua ni kwa nini una shindwa kunia.”

Makamu wa raisi mwili mzima unamtetemka kwani siri hii haifahamu kabisa na mafunzo ya kininja yalitufanya tujifunze imani za kishetani zinazo tufanya tuwe na uwezo huu.

“U…mef…..fanya..je f…anya….je?”

Makamu wa raisi aliiuliza huku akiwa na kigugumizi cha hali ya juu.

“Nilicho kifanya nimekifanya hivyo usiulize nina fanya nni. Ila waambie watu wako wote wakae mbali na familia yangu. Oya unapenda kuishi?”

“N…di…o”

Mlinzi huyu niliye muweka upanga shingoni mwake alizungumza huku akitemeka mwili mzima.

“Leo naondoka sijamwaga damu y ahata mmoja wenu. Siku nikirudi nikiwa kama hivyo basi mujue nina waua wote”

Nikatoa gololi moja ndogo ambayo ukiipiga chini ina pasuka na kutoa moshi mwingi sana una walevya maadui na kuwafanya wazubae zubae. Nikaipiga chini kisha nikatoka ndani hapa kwa kasi sana. Nikarudi eneo alipo Ruben na nikaingia ndani ya gari.

“Vipi kwema mkuu?”

“Kwema, turudi Bagamoyo”

“Sawa”

Safari ikaanza huku ukimya ukitawala ndani ya gari hili.

“Hahakudhuru”

“Hawezi”

“Sawa sawa mkuu”

“Saa ngapi sasa hivi?”

“Tisa kasoro”

“Sawa, ongeza mwendo”

Ruben akaongeza mwendo na tukawahi kufika Bagamoyo kwenye nyumba yangu ya siri. Nikarudisha mavazi hata sehemu nilipo yatoa. Nikavaa mavazi yangu na nikatoka nje na kuingia ndani ya gari na safari ya kurudi ikulu ikaanza.

“Usije ukamuelez amtu yoyote kwa chochote kilicho tokea leo”

“Sawa muheshimiwa raisi”

Tukafika ikulu, jinsi tulivyo toka ndivyo jinsi tulivyo ingia.

“Kwa sasa kapumzike tuta onana asubuhi”

“Sawa muheshimiwa”

Nikaingia ninapo ishi, nikapitiliza moja kwa moja hadi chumbani kwangu. Nikamkuta Cauther akiwa amepitiwa na usingizi, nikaingia bafuni na nikaingia katika sinki kubwa la kuogea huku kwa mara kadhaa nikijaribu kutafakari ombi alilo niambia makamu wa raisi.

‘Nchi sio yangu hii , ila hii ni familia yangu’

Nilizungumza kimoyo moyo. Nikaoga, nikajifunga taulo na kurudi chumbani kwangu, nikamtazama Cauther pamoja na mtoto wangu. Wote wamelala kwa pamoja. Nikachukua simu yangu juu ya meza na nikawapiga picha kadhaa kisha nikalala pembeni yao.

‘Kweli nikishuhudia mke wangu akiuwawa mbele yangu nita umia?’

‘Eddy’

Niliihisi sauti ikiniita nafsini mwangu na nikajikuta nikitulia kimya.

‘Eddy’

‘Eehee’

‘Usiruhusu makamu wa raisi kuwa raisi’

‘Nani wewe una niongelesha?’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikikaa kitako kitandani kwa mana hili nalo ni jipya kwenye maish yangu.

‘Uta jua mimi ni nani baadae ila usiruhusu hilo litokee. Una jua ni nini atakacho kifanya mara baada yaw ewe kuwa raisi?’

‘Hapana?’

‘Ata kuwa na nguvu na mtu wa kwanza kukuwinda ni wewe na familia yako. Ata waua hakikisha mgombea uraisia na lindwa kuliko hata wewe mwenyewe na hadi awe raisi ndio uweze kumuondolea uangalizi’

‘Ila wewe ni nani?’

‘Kila binadamu ana malaika, malaika mzuri na mbaya. Katika nafsi za binadamu huwa kuna roho mbili, roho ya kuonya na roho ya kukushawishi. Watu wanao mjua Mungu wana weza kuelewa hili una weza kumuuliza mchungaji wako’

‘Ina maana wewe ni malaika?’

‘Ndio hata hichi tunacho kizungumza mke wako hakisikii na unayo niuliza mke wako hasikii.

‘Je familia yangu itakuwa salama nikimlinda huyu mgombea?’

‘Ndio’

‘Una uhakika?’

‘Sisi sio kama binadamu, tuna uwezo wa kujua yaliyo mbele na nayanayo kuja mbeleni mwa mwanadamu. Ulicho muonyesha leo kime mfanya aweze kukufikiria mabaya kufikiria ni namna gani atakavyo kumaliza. Usimuamini mtu ambaye amefanya mauaji ya watu wengi na watu wako wa karibu’

‘Kwa hiyo nimefanya kosa kumuacha hai?’

‘Hapana?’

‘Ila?’

‘Waovu siku zote huwa wana pewa muda mkubwa sana wa kuishi?’

‘Kwa nini?’

‘Kwa sababu wana paswa kujua makossa yao ili wamrudie mwenuezi Mungu’

Nikamtazmaa mwanangu na kumuona akitabamu japo amelala katikati yetu.

‘Mwanao ana niuona’

‘Nini?’

‘Watoto wadogo wana uwezo mkubwa wa kuwaona waovu na malaika ndio maana una muona ana tabasamu’

‘Sasa niambie ni nini nina paswa kufanya?’

‘Nimecha kueleza, cha kufanya ni kuhakikisha kwamba makamu wa raisi hawezi kuingia madaerakani’

‘Sawa’

‘Nikutakie mapumziko mema’

‘Ngoja kwanza’

‘Ndio’

‘Nitakuwa nawasiliana na wewe vipi?’

‘Nitakapo ona haja ya moyo waku kunihitaji nita kuwa nina kuja’

‘Kwa hiyo una nihakikishia familia yangu kuwa salama?’

‘Ndio’

‘Haya’

Nikamtazama Nadia na kumuona akirusha rusha vimikono vyake na miguu huku akioenkana kutulia na baada ya muda akatulia huku kidole chumba cha mkono wake wa kulia akikiweka mdomoni mwake na akaendelea kuuchapa usingizi na kunifanya nitabasamu. Usingizi ukanipitia na nikalala fofofo.

Mlio wa simu yangu ukanifanya nifumbue macho, nikatazama chumba kizima na kukuta mwanga wa jua ukiwa umesha tawala. Cauther akaingia ndani hapa akiwa amembeba mtoto.

“Vipi mume wangu?”

“Salama honey”

Cauther akanikabidhi simu yangu huku akinipiga busu la mdomo. Nikatazama simu hii na ina toka kwa Ruben.

“Ruben”

(Karibu nikuunge kwenye group la hadithi ya AIISSII u kill me chapter four. WhatsApp 0657072588. Ada ni 4000 kwa mwezi. Karibu sana)

“Za asubuhi muheshimiwa raisi”

“Salama”

“Upo sehemu nzuri?”

“Ndio, nipo kitandani na simu yako ndio imenistua”

“Mkuu kuna tatizo”

“Tatizo gani?”

“Mshauri wako na mgombea uraisi wa chama kilichopo madarakani, amepata ajali mbaya sana katika msafara wake wa kampeni na gari yake ayo imepondeka kiasi kwamba sidhani kama ametoka akiwa hai”

Nikajikuta nikistuka sana na kukaa kitako kitandani hadi mke wangu akashangaa kwa maana ajali hii ni ya kupangwa na huyu mshenzi makamu wa raisi na kama mshauri wangu akifa haki ya Mungu makamu wa raisi ni lazima na yeye afe.



(Karibu nikuunge kwenye group la hadithi ya AIISSII u kill me chapter four. WhatsApp 0657072588. Ada ni 4000 kwa mwezi. Karibu sana)

“Amepelekwa hospitali gani?”

Nilizungumza huku jasho likinimwagika mwilini mwangu.

“Kwa sasa ana pelekwa Muhimbili wapo njiani”

“Sawa nini kwenda Muhimbili sasa hivi. Wapigie na msafara wangu uandaliwe haraka iwezekanavyoNi

“Sawa mkuu”

Nikakata simu na kuiweka pembeni.

“Mshauri wangu amepata ajali”

“Mungu wangu, ajali ya nini?”

“Gari walikuwa kwenye msafara yaani. Daa ina tia hasira sana mzee wa watu mimi ndio nilimuomba kuingia kwneye siasa na sasa hivi hali yake ina kuwa kama hivyo kwa kweli ina kera sana”

Nilizugumza huku nikikimbilia bafuni, nikaoga haraka haraka na kurudi chumbani na kukuta nguo zangu zikiwa zimesha andaliwa na mke wangu na kuwekwa juu ya kitanda. Nikavaa haraka haraka, Cauther akanitengeneza vizuri shati langu.

“Nakuomba uwe makini mume wangu na Mungu akutangulie”

“Amen. Mubaki salama wewe na mtoto”

“Amen”

Nikambusu mke wangu mdomoni kisha nikatoka ndani hapa. Nikaingia katika gari langu na safari ya kuelekea hospitali ya Muhimbili ikaanza. Nikaishika simu yangu mkononi nikatamani kumpigia makamu wa raisi ila nikajikuta nikivumilia hadi nitakapo muona mshauri wangu. Tukafika Muhimbili na kukuta mazingira ya hospitali yamesha wekwa chini ya ulinzi mkali. Nikapokelelewa na daktari mkuu msaidizi wa hospitali hii na moja kwa moja tukaanza kueleka katika chumba cha matibabu.

“Vipi hali yake?”

“Ahaa hali yake sio mbaya sana”

“Ina maana hajaumia sana?”

“Ndio mkuu”

Tukafika katika chumba hichi na nikaingia ndani na kumkuta mshauri wangu akiwa amekaa ktandani.

“Mkuu umekuja?”

“Yaa nimekuja niambie mzee wangu shikamoo”

“Marahaba”

“Vipi imekuwaje?”

“Tunaombeni chumba”

Mshauri wangu alizungumza na madaktari wakatoka ndani hapa.

“Eheeh niambie”

“Aisee ilikuwa gari ya mbele yetu kwneye msafara ilipasuka tairi ya nyuma na kama unavyo fahamu gari zinakuwa kwenye mwendo wa kasi”

“Ndio ndio”

“Hivyo dereva alijaribu kuikwepa ile gari ya mbele ila kwa bahati mbaya ilishindikana na gari ikaanza kubingirika mara kadhaa na gari imepondeka kisawa sawa”

“Kwani gari unayo itumia sio bullet proof?”

“Ni bullet proof ila kwenye ajali bwana chochote huwa kina weza kutokea pasipo kutegemea ubora wa gari uliyo nayo.”

“Sasa una jisikiaje?”

“Mimi nipo fiti kabisa. Yaani hapa ninahitaji kuendelea na safari ya kampeni. Nimaagiza helicopter kuletwa hospitali na niendelee na kampeni”

“Aisee Ruben aliniambia gari yako ime pondeka pondeka sana na nikajawa na wasiwasi mkubwa sana”

“Ni kweli ime pondeka. Ila ingekuwa sio kupita maeneo maeneo, aisee ningekuwa nimesha kufa.”

“Weee”

“Ndio, kabla ya kuingia huku kwenye sisas nilienda sehemu huko kushuhulikiwa. Yaani kama ni ajali ya kutumwa basi imenishinda.”

“Hapo ndipo ninapo kupendea”

“Na ina bidi na wewe ni kupeleke huko. Kuna wazee wa Kisukuma wapo vizuri wana kupa mambo hadi wewe mwenyewe una kubali. Ona nimetoka na nimechubuka chubuka tu. Ila dereva nasikia hali yake sio nzuri pamoja na mlinzi wangu naye hali amevunjika mguu”

“Aisee hapo nimekukubali mzee wangu”

“Hivyo ndivyo inavyo paswa kuwa ndugu yangu. Haya ni maisha na kwenye siasa huku kuna mambo mengi sana mabaya. Usipo komaa, una kufa kwa kweli”

“Yaa ni kweli ndugu yangu”

Mshauri wangu akasimama wima na kajinyoosha nyoosha viongo vyake. Akanitazama usoni mwangu na akanishika bega langu la mkono wangu wa kulia.

“Nilikuahidi kwamba nita hakikisha kwamba nina uchukua uraisi. Siwezi kukuangusha wala kuukosa”

“Nashukuru na kuna jambo moja ambalo jana nililifanya na sikukuambia”

“Jambo gani?”

Tukaka kitandani.

“Jana nimekutana na makamu wa raisi majira ya saa sita usiku alinipigia simu na akaniomba niweze kuonana naye kule kwake”

“Vipi hukufanya chochote?”

“Nilihitaji kumuua ila alinisisitizia sana kuhusiana na familia yangu. Pia alihitaji nimsafishe jina ili awe raisi”

“Mshenzi sana yule ana hisi ni nani atakaye mpa kura?”

“Yaa nilimuambia hivyo. Una jua saa nyingine najuta kwa nini nimekuwa na familia. Kwani nina shindwa kufanya maamuzi kutokana na kuhofia maadui kuiangamiza familia yangu”

“Ngoja nikuambie jambo moja Eddy”

“Ndio ndio”

“Hapa nina zungumza kama baba kwa maana nina watoto wakubwa zaidi yako”

Nikajikuta nikutabasamu.

“Baba mzuri siku zote ni yule anaye hakikisha kwamba familia yake ina kuwa salama na kuwa mbali sana na maadui zake. Umefanya maamuzi sahihi kuwa na familia kwa mana una weza kutofautisha maisha iliyo kuwa una ishi bila ya Cauther na maisha ya sasa unapo kuwa na Cauther pamoja na mwanao Nadia.”

“Pia umefanya maamuzi sahihi ya kuto kumuua kwa maana ange idhuru familia yako na ingekuwa una jisikia vibaya sana na ikitegemea huna hata miaka mitano katika ndoa”

“Ni kweli”

“Sasa hivi wewe dili na familia yako. Sasa hivi wewe hakikisha kwamba familia yako ina isha vipi. Now niachie hii game. Mimi ndio mchezaji kwenye hili sasa. Naijua hii nchi na nina mjua yule mshenzi toka akiwa hana mbele wala nyuma hadi hapo alipo fika. Hivyo ameniwinda nami nita muwinda kimya kimya. Nikuahidi tu, hawa sijui scorpion wata teketea, ngoja nichukue madareaka uta jua hilo”

“Nashukuru sana”

“Nakuandalia nafasi ya wewe kurudi kuwa kiongozi wa nchi hii tena. Una passion ya kuwa kiongozi na una uwezo huo, hivyo hakikisha una kuwa makini kwenye kila hatua uan nielewa?”

“Ndio nina kuelewa”

“Jambo jengine kabla sija sahau”

“Ndio”

“Nahitaji sasa hivi udili sana kwenye ujenzi wa lile eneo ulilo nunua kule India. Wewe na mke wako mujali sana maisha yenu baada ya huu mwenzi kuisha”

“Sawa sawa”

Mshauri wangu akachukua koti lake la suti na kulivaa vizuri.

“Lazima nishinde na nikupe siri moja”

“Siri gani?”

“Yule mpuuzi ana niogopa sana na nina jua hawezi kunifanya chochote ndio maana alikuita wewe kukuomba umsafishe akiamini una weza kunigeuka pasipo kujua ni yapi tuna muwazia”

“Ni kweli. Mimi nikushukuru kwa kunielewa”

“Nina kuelewa sana Eddy, kulilo watu wote kwenye lile jengo jeupe, ukimtoa Cauther kwani yeye ndio ana kuelewa zaidi sana”

“Yaa”

(Karibu nikuunge kwenye group la hadithi ya AIISSII u kill me chapter four. WhatsApp 0657072588. Ada ni 4000 kwa mwezi. Karibu sana)

Nikaka kimya kidogo.

“Huwa una amini juu ya mambo ya kuongea na malaika?”

“Kivipi sija kuelewa swali lako”

“Yaani ipo hivi, jana mimi nilizungumza na malaika, sijui ndio malaika kweli au laa. Aka nisisitizia sana nisimruhusu makamu wa raisi kugombania uraisi sasa nashindwa kutambua ni malaika kweli au mizinguzi ya mawenge mawenge”

“Hahaa siwezi kusema ndio au hapana kwa maana ni hali ya kiriho zaidi. Swali hilo litakuwa zuri sana endapo uta zungumza na mchungaji wako wa kanisa”

“Na kitambo sana sijakwenda kanisani?”

“Kwa mikimbizano hii sio rahisi kuhudhuria misa zote za kanisani.”

“Ina bidi nikutoka hapa niende kanisani”

“Ni jambo la heri pia”

Mlango ukagongwa.

“Ingia”

Akaingia mlinzi wa mshauri wangu.

“Muheshimiwa helicopter imesha fika”

“Sawa nina kuja”

“Hawa vijana wapo vizuri?”

“Yaa wapo vizuri sana na nina wafahamu ni wa kipindi kirefu”

“Sawa sawa ni jambo zuri”

“Sasa muheshimiwa raisi kwanza nikushukuru kwa kujali na kuja kuniona na jengine nikuombe nikakimbizane na ratiba za uchaguzi japo nipo nyuma kwa masaa kadhaa”

“Usijali ndugu yangu. Nenda kapambane na hakikisha kwamba tuna muonyesha huyu mpuuzi kwamba sio kila ndoto lazima itimizwe hata kama umeiandaa kwa kipindi gani”

“Ana ndoto gani?”

“Kuwa raisi, ana dai ndio ndoto yake”

“Hahaa Mungu pia hawezi kumpa uraisi mtu ambaye matendo yake ni maovu katika nchi”

“Ni kweli aisee.”

“Pia ana dai ana weza kufanya tukio mara baada yaw ewe kuapishwa?”

“Hizi ni propaganda Eddy wala asikutishe na kukuogopesha, nitakapo kuwa raisi wata juta. Yaani mission yangu ya kwanza ni kuhakikisha kwamba mkuu wa Scorpion na watu wake wana teketea”

“Sawa sawa”

Tukatoka ndani hapa na mshauri wangu akaelekea kwenye kiwanja cha helicopter huku nami nikielekea katika magari ya msafara wangu pamoja na walinzi wnagu.

“Nahitataji kuelekea kanisani”

“Kanisa gani mkuu?”

Nikamtajia mlinzi wangu huyu kanisa ninalo kwenda. Nikatoa simu yangu mfukoni na nikampigia mchungaji aliye nifungisha ndoa mimi na mke wangu.

“Haloo nipo kwenye maombi?”

Mchungaji alizungumza kwa sauti ya chini kidogo.

“Ni mimi Eddy, Raisi”

“Muheshimiwa raisi”

“Ndio ni mimi ila kama upo kwenye maombi endelea. Si upo kanisani?”

“Ndio ndio mwanangu”

“Nakuja”

“Sawa”

Nikakata simu. Tukafika kanisani hapa, walinzi wangu wakaimarisha ulinzi eneo zima la kanisa, wakalikagua kanisa kisha nikaruhusiwa kuingia ndani. Nikaketi kwenye benchi la mbele kabisa na baada ya dakika kama ishirini mchungaji akaingia kanisani hapa akitokea ofisini kwake.

“Karibiu sana Eddy”

“Nashukuru sana baba”

Tukakumbatiana na mchungaji huyu ambaye kipindi nilipo toka kwenye kazi yangu ya kijeshi alikuwa ni mshauri mkubwa sana kwangu kuhakikisha akili yangu ina rudi kwenye ubinadamu kwani nilikuwa ni mtu mwenye hasira na uchungu mkubwa utokanao na kuuwawa kwa wanajeshi wezangu.

“Mungu amejibu maombi yangu. Tuketi”

Tukaa kwenye benchi hili. Huku walinzi wangu wakiwa wamezagaa kanisani hapa.

“Ni kweli mchungaji”

“Vipi mke wako na mwanao wana endeleaje?”

“Wana endelea vizuri kwa kweli na ninamshukuru Mungu kwa uwepo wapo wao kwenye maisha yangu”

“Hilo ndip jambo la msingi. Halafu mlete bwana binti abatizwe”

“Sawa sawa nita mleta mchungaji”

“Niambie mwanangu umekuja kufanya nini?”

Mchungaji aliniuliza kwa sauti ya upole huku akinidadisi machoni mwangu. Nikaka kimya kwa sekunde kadhaa huku nikimtazama machoni mwake.

“Mimi ni mtu mbaya baba mchungaji”

“Una maana gani kusema hivyo?”

“Uwepo wangu madarakani, ume pelekea watu wengi kuuwawa, kwa mfano wale walio kuwa kanisani, ajali za ndege. Zote nina hisi kwamba maadui zangu walizitumia ili kunikamata mimi”

“Eddy Eddy Eddy mwamangu. Usifadhaike moyoni mwako uka hisi labda wewe ndio una husika kwenye zile ajali. Ile ni mipango ya shetani juu ya taifa la Mungu. Kiongozi yoyote mwenye nguvu ya Mungu ndani yake huwa hakosi maadui. Hata ukitazama kwenye vitabu vya Mungu, wafalme wote walio kuwa wana ongoza mataifa makubwa, walikuwa na maadui. Maadui ambao walikuwa ni watu wa kuzivamia ngome za mataifa hayo na kujaribu kuziteka. Ila wanapo simama imara zile ngome zina tetewa kwa kumwagika damu na kupotea kwa maisha ya watu. Hivyo ndivyo ilivyo kwenye dunia ya sasa hususani kwenye hii nchi ya Tanzania”

“Hivi Mungu hawezi kuzuia majanga makubwa kama hayo?”

“Hahahaha ina wezekana kuzuiwa ila Mungu ana hitaji kuwakumbusha wanadamu kwamba wana ishi kwenye dunia yenue uovu mkubwa. Dunia ambayo muovu shetani ana zingira zingira ili mradi kuleta machafuko”

“Je huyu anaye gombania uraisi kwa niaba yangu. Ni mtu sahihi wa kuiongoza hii nchi?”

“Ndio”

“Kweli?”

(Karibu nikuunge kwenye group la hadithi ya AIISSII u kill me chapter four. WhatsApp 0657072588. Ada ni 4000 kwa mwezi. Karibu sana)

“Ndio ni mtu sahihi nan chi ita kuwa salama chini yake. Ana jua hili taifa na maadui wa hili taifa hivyo ata shuhulika nao kisawa sawa”

Nikashusha pumzi nyingi huku nikimtazama mchungaji.

“Baba mchungaji”

“Naam mwanangu”

“Nahitaji uanza maisha mapya. Nahitaji kuwa mti mwema zaidi ya jana. Nahitaji kuwa yule Eddy ambaye ulinibadilisha na kunifanya niweze kuijua na kuipenda dini. Tafadhali baba nahisi nime kengeuka kutokana na ubize wangu, hivyo nakuomba sana baba mchungaji”

“Hayo ni maamuzi mazuri sana mwanangu kwani sisi binadamu tumeumbwa kwa kufanya makossa ili tuje mbele za Mungu na kumuomba msamaha. Kabla ya kufanya toba nita kuomba mama naye aje hapa kwa ajili ya kuwaombea kwa pamoja na ikiwezekana tumbazite na mtoto”

“Sawa sawa mchungaji”

“Mwanao ana itwa nani?”

“Nadia”

“Kwa nini umempa jina hilo?”

“Ahaa ni kutokana na babu yake kuomba nimapatie jina hilo”

“Tafadhali, epuka sana kumpa mwanao jina la kurithi kwa mtu. Mchagulie jina lako kutoka moyoni kwani litakuwa ni baraka na mwanga katika maisha yake”

“Kwani jina la kurithi ina madhara?”

“Makubwa sana. Ubaya wa haya majina huwa yana fwata na tabia za yule aliye kuwa na jina hilo. Kama laikuwa ni malaya na mpenda waume za watu pasipo kujali ata waumiza vipi wale wenye waume zao watakapo tambua ukweli basi ata mwanao naye ata kuwa na tabia hizo”

Nikashusha pumzi nyingi huku nikimtazama mchungaji kwani hata Nadia mkubwa ambaye ni shemeji yangu. Ana mahusiano ya kimapenzi na mimi pasipo kukali mimi ni mume wa dada yake tena wa tumbo moja na anacho kijali yeye ni starehe ya mwili wake basi. Mchungaji akanishika mkono wangu wa kulia kisha akafumba macho na kaunza kuomba nami nikafumba macho. Baada ya dakika tano akasema ame.

“Eddy”

“Naam baba”

“Naona roho ya mauti ina zunguka juu ya familia yako. Mwangu hii ni hatari sana ina bidi ufanye jambo juu ya hili”

“Una maanisha nini baba mchungaji”

“Nina ona malaika mtoa roho akizunguka juu ya familia yako. Ana taka kuondoka na roho ya mmoja wenu. Ina weza ikawa wewe, mke wako ua mwanao hivyo ni hatari sana hii roho ikiendelea kuzunguka juu ya maisha ya familia yako mwanangu”

Mapigo ya moyo yakaanza kunienda kasi kwa kweli, woga ukanijaa kwani kwenye maisha yangu hakuna kitu ninacho kiogopa kama kifo, husani kwa wana familia wangu, ni heri nikaanza kufa mimi kuliko nikashuhudia wana kufa wao.



“Hiyo roho haiwezi kuondoka?”

“Kama nilivyo sema una weza kumuita mke wako na mwanao wakaja hapa kanisani na nikawafanyia maombi”

“Dakika moja”

Nikamuita mlinzi wangu kwa ishara. Tukasimama pembeni.

“Ndio muheshimiwa”

“Nahitaji familia yangu iweze kufika hapa kanisani”

“Sawa muheshomiwa raisi ila ngoja nifanye mawasiliano”

“Sawa”

Nikarudi katika bechi niliko kuwa nimekalia.

“Una mpango gani baada ya muda wako wa uongozi kuisha?”

“Nahitaji kupumzika mimi na familia yangu, sihitaji mikwaruzano na majukumu ya kimchi. Majukumu ninayo yahitaji sasa hivi ni majukumu ya familia yangu”

“Ni maamuzi mazuri na Mungu akupiganie”

“Amen”

Mlinzi wangu akanifwata na nikanyanyuka ili nimsikilize.

“Sahamani muheshimiwa raisi, kutokana na swala la kiusalama hatuwezi kuileta hapa familia yako na pia tuna omba uweze kurudi ikulu.”

“Sawa nimekuelewa”

Nikaka katika benchi huku nikimtazama mchungaji.

“Kwa hali ya usalama familia yangu haiwezi kufika hapa. Nina kuomba kama uta pata muda uje ikulu kunifanyia maombi”

“Hakuna shaka katika hili Eddy mwanangu. Nitakuambia ni lini nawe uweze kujiandaa”

“Sawa”

Nikapeana mkono na baba mchangaji kisha nikatoka kanisani hapa, nikaingia dani ya gari na tukaondoka kanisani hapa.

“Kuna ishu gani inayo endelea?”

Nilimuuliza mlizi wagu mara baada ya kushusha kioo kinacho tutenganisha kati yangu na dereva pamoja na mlinzi wangu aliye kaa siti ya mbele pembeni ya dereva.

“Kwa jinsi ajali ya mgombea uraisi ilivyo tokea tuna ona ni swala la kupangwa hivyo hatujui ni nini kinacho weza kupangwa kwako”

Simu yangu ikaanza kuita. Nikaitoa mfukoni na kuona namba ya makamu wa raisi. Nikapandisha kioo hichi na kuipokea.

“Naona emepunyuka kwenye hili”

“Ina maana wewe ndio uliye panga?”

“Nina imani kwamba jana tulisha zungumza hili na nina imani kwamba umelielewa.”

“Nisikilize nchi kama nchi haiwezi kuongozwa na mwenda wazimu kama wewe”

“Eti ehee?”

“Ndio na unacho kifanya ni makosa. Jana umeona nilicho kifanya sasa usijaribu kufanya upumbavu, nita kusaka na nita kuua kwa mikono yangu. Sasa umenitengeneza wewe na angalia sana nisije nikakuharibu”

“Niliamini kwamba hili tuta limaliza kiusalama mimi na wewe ila naona hutaki tulimalize salama. Subiri uta ona”

Simu ikakatika na kunifanya nishushe pumzi kidogo kwa maana ni jambo linalo kere kuendelea kubishana na mzee huyu. Tukafika ikulu na moja kwa moja nikaelekea ninapo ishi na familia yangu.

“Vipi mume wangu, nimememuona mzee akiendelea na kampeni zake?”

“Ndio ilikuwa ni ajalai ya kawaida na ana endelea vizuri”

“Mungu ni mwema kwa kweli”

“Yaaa vipi upo salama?”

“Mimi nipo salama tu mume wangu, hofu ni kwako”

“Nimerudi na nilionana na baba mchungaji ana waswalimia sana wewe na mtoto”

“Ohoo tuna shukuru sana. Baadae nita mpigia nizungumze naye”

“Sawa mke wangu”

Baada ya siku mbili baba mchungaji akafika ikulu hapa na akatuombea sala iliyo garimu lisaa zima.

“Sasa moyo wangu una amani na nina imani Mungu ata endelea kuwalinda sasa na hadi baadae”

“Amen”

“Jambo la msingi ni kuhakikisha kwamba muna ishi katika njia na misingi inayo mpendeza Mungu”

“Amen”

Tukapata chakula cha usiku na baba mchungaji kisha akaondoka. Shuhuli za kampeni zika zidi kusonga mbele hadi siku ya uchaguzi ikawadia. Ukimya wa makamu wa raisi kwa kipindi hichi chote ukanifanya niwe ni mtu wa wasiwasi kwa maana sijui ni jambo gani analo lipanga. Mimi na mke wangu tuka piga kura ya kumchagua bwana Leonard Simba, huku muitikio wa watu walio jitokeza kupiga kura ukiwa ni mkubwa sana. Hesabu za kielectotonic zina onyesha hadi sasa hivi kura alizo pigiwa bwana Simba ni milioni thelathni na mbili sawa na asilimia stini na sita huku akiwaacha mbali sana wapinzani wa vyama vingine.

“Una kuwa raisi mzee wangu?”

“Namshukuru Mungu kwa hili kwa maana nilkuwa mshauri wa maraisi watatu. Sasa nina imani ni wakati wa mimi kuongoza kile nilicho washauri”

“Ni kweli. Ila nina jambo moja ambalo nina lifikiria sana na nina kosa jibu”

“Jambo gani?”

“Kuna swala la makamu wa raisi. Nina ona ametulia sana na sijui ana mpango gani ana upanga nyuma ya ukimya wake”

“Usijali Eddy serikali ninayo kwenda kuiunda mimi itakuwa sio ya mchezo mchezo. Na itaendesha oparesheni za siri sana kuhakikisha tuna mpata na kile kitengo cha X ulicho kipendekeza kita pita na NSS ita kwenda kuzikwa”

“Nashukuru sana kwa hilo”

“Kikubwa tuombeane kwa Mungu”

“Mungu ni mwema ata bariki”

“Amen”

Muda wa matokeo kutangazwa ukawadia na bwana Leonard Simba akashinda kwa asilimia themanini na tano huku hizo asilimia kumi na tano zilizo baki zikigawanywa gawanywa kwa vyama vya pinzani. Shangwe na furaha zikatawala katika ofisi hii tuliyopo kwani tulikuwa tuna subiria matokeo haya kwa hamu kubwa sana.

“Hongera sana raisi mtele”

“Nashukuru sana muheshimiwa raisi”

Shangwe zikazidi kutawala mitaani huku wananchi wengi wa chana hichi wakifurahia juu ya matokeo haya ambayo ni matokeo yaliyo vunja rekodi nyingine kwenye hili taifa toka lilivyo kuwa na vyama vingi ni maraisi wachache sana waliweza kushinda kiti cha uraisi kwa kupata asilimia themanini na kuendelea, za kura zote zilizo pigwa. Nyumba yangu niliyo inunua kipindi ni jenerali wa jeshi ikafanyiwa ukarabati mwengine huku ikiwekewa vifaa malumu vya ulinzi kwa maana nina kwenda kuishi kama raisi mstafu. Japo sina mpango wa kukaa Tanzania kwa kipindi kirefu ila ni lazima ulinzi wangu na familia yangu uimarishwe. Nikaletewa kitabu maalumu chenye ramani ya nyumba baada ya maboresho na injiani mkuu wa serikali.

“Muheshimiwa raisi hii ndio nyumba yetu mpya inavyo onekana kwenye ramani. Kuna internal channel ambazo endapo kuta tokea jambo lolote la uvamizi wewe na familia yako muna weza kukimbia. Pia kuna yumba nyingine ndogo tume iongozea chini ya ardhi katika nyumba hiyo. Nyumba hii ni eneo ambalo endapo kuna uvamizi huku juu, wewe na familia yako muna weza kuingia katika nyumba hiyo na imejengwa kwa umara ambao una weza kuhimili mitetemeko yote ya ardhi, pia haina bomu la ina yoyote linaweza kuingia.”

“Nashukuru sana nyumba mume iboresha sana”

“Ni ujenzi wa kisasa muheshimiwa raisi. Pia milango, pamoja na madirisha yote hatapitishi risasi. Kwenye kuta za nyumba yako tumeweka system ya geti za chuma ambapo kunapo tokea tatizo una weza kuikoctrol nyumba yako iweze kujifunga yote”

“Nicontrol vipi?”

“Kuna hii ipad ina system ambayo una weza control kila system ya nyumba yako”

“Kwenye simu yangu ya kawaida hamuwezi kuiweka?”

“Ina wezekana muheshimwia raisi jambo la msingi ni kuhakikisha kwamba simu yako haipotei”

“Hilo halina shaka”

Injiania huyu mkuu akanielekeza kila kitu. Siku iliyo fwata tukaelekea katika nyumba yetu mimi na mke wangu na tukakagua kila kitu.

“Sasa mume wangu hii nyumba si tuibebe tuendenayo India”

“Hahahaa ingekuwa ina wezekana tunge ibeba”

“Ila imekuwa nzuri sana mume wangu, wame ibadilisha sana tofauti na ilivyo kuwa pale mwanzano”

“Yaa wameibadilisha na imekuwa nzuri”

Baada ya kujiridhisha tukarudi ikulu huku tukisubiria siku ya kuapishwa kwa raisi mpya na ndio siku ambayo uongozi wangu wa muda nilio ushikilia una kwisha. Kila kitu kinacho husiana na ofisi ya raisi tayari nimesha vikabishi kwa raisi mpya bwana Simba.

Siku ya kuapishwa kwa raisi mpya ikawadia. Kama kawaida wananchi wengi wakajitokeza katika siku ya kuapishwa kwa raisi mpya katika kiwanja kikubwa cha mpira wa miguu. Ulinzi wa kila aina umeimarishwa katika eneo hili huku mimi nikiwa ndio kiongozi wa mwisho kufika kiwanjani hapa. Baada ya kufika nikakagua gwaride kwa mara ya mwsiho kisha shuhuli za kuamuapisha raisi mpya zikaanza. Raisi Simba akaapishwa rasmi na kuwa raisi wa nchi hii. Huku nami nikiwa sasa ni raisi mstafu. Msafara nilio jia nao mimi ndio akaondoka nao raisi Simba mara baada ya shuhuli hizi kumalizika kisha nami nikaingia katika msafara mwengine na kuondoka kiwanjani hapa. Nikarudi ikulu ambapo ndipo alipo elekea raisi Simba.

“Sasa uwanja ni wako muheshimiwa raisi”

Nilizungumza huku nikitabasamu.

“Ni kweli, umetenda kazi kubwa sana kijana. Miezi mitatu uliyo shikilia nchi sio haba”

“Yaa ni kweli”

Tulizungumza huku tukiwa ndani ya ofisi tukiwa sisi wawili.

“Ila umri wako una ruhusu kulitumikia taifa. Je utakapo kuwa tayari ni nafasi gani una hitaji kuishikilia hapa nchini?”

Nikashusha pumzi huku nikitazama picha mpya ya raisi Simba ikiwa imebandikwa hapa ofisini, kabla ya picha hii kulikuwa na picha yangu.

“Kusema kweli bado sija fikiria. Ila kama uta hitaji ushauri wa maswala ya kiusalama wa nchi basi usisite kuniambia”

“Sawa hakuna shaka.”

“Utaishi Tanzania au India?”

“India”

“Utahitaji ulinzi wa kukulinda hadi huko?”

“Hapana, mimi mwenyewe ni komandoo wa kutosha hivyo nahitaji kuwa mwenyewe na mke wangu pamoja na mwanangu”

“Sawa Eddy nikutakie maisha mema na burudika”

“Nashukuru. Ila kumbuka makamu wa raisi ana kiwinda hichi cheo hivyo kuwa makini naye”

“Usijali Eddy nipo makini sana”

“Nafurahi kusikia hivyo”

Baada ya mazungumzo haya tukatoka ofisini hapa. Mimi na mke wangu tuka agana na wafanyakazi wa ikulu ambao wengi wao walituzoea sana hususani wapishi.

“Mungu awabariki tuta onana”

Nilizungumza huku machozi yakinilenga lenga. Japo nimekaa nao kwa muda mfupi ila nilikuwa ni mtu wa kuzungumza nao vizuri. Tukaelekea katika kiwanja cha helicopter ya raisi, tukawapungia kwa mara ya mwisho waafanyakazi na baadhi ya waandishi wa habari wa ikulu wanao endelea kurekodi namna tunavyo ondoka ikulu. Tukaingia ndani ya helicopter na nikamkuta shemeji Nadia akiwa na mtoto wetu Nadia.

“Shem ndio hatuji tena ikulu?”

Swali la Nadia likanifanya nitabasamu huku nikimtazama.

“Umepapenda?”

“Ndio sijawahi ona sehemu nzuri kama ikulu”

“Usijali kwa miaka mingine mwenyezi Mungu atakapo tujalia tuta rudi”

“Kweli shem”

“Ndio”

Taratibu helicopter hii ikaanza kunyanyuka huku helicopter nyingine zinazo fanania na hizi ambazo jukumu lake ni kumlinda raisin azo zikanza kunyanyuka na kuiweka helicopter hii katikati na safari ya kuondoka eneo hili ikaanza.

“Asante Mungu tumemaliza salama”

Cauther alizungumza huku akinishika kiganja cha mkono wangu wa kulia.

“Ni kweli mke wangu, Mungu ni mwema ametusaidia”

“Nakupenda sana Eddy”

“Nakupenda pia mke wangu”

Taratibu Cauther akanibusu katika lispi zangu huku tukitazama Mandhari ya bahari tunayo ivuka na kuelekea Kigamboni ilipo nyumba yetu ambayo iliongezewa matengenezo na serikali tofauti na pale awali tulivyo inunua. Eneo la nyumba hii pia lime ongezwa kwa kiasi kwamba kuna viwanja vya viwili vya michezo, kuna kiwanja kikubwa cha helicopter na kina baadhi ya bustani nzuri zilizo tengenezwa kwa ustadi wa hali ya juu. Helicopter zikashuka katika kiwanja hichi cha nyumba yetu. Tukashuka ndani ya helicopter na tukapokelewa na Willy pamoja na Gody.

“Karibu sana nyumbani”

“Mumefika saa ngapi?”

(AIISSII YOU KILL ME CHAPTER FOUR(Killer) inazidi kusonga mbele. Wahi sasa ujiunge kwenye group WhatsApp 0657072588 kwa sh 4000/= tu.

Karibu sana)

“Toka asubuhi tupo hapa tuna andaa nyumba”

“Hahahahaa”

“Shem karibu kwenye maisha mapya bwana”

“Asante Willy ila tulikwenda kutalii tu pale hapa ndio nyumbani sasa”

“Ni kweli”

Tukaingia ndani na kukuta seble ikiwa imepambwa kana kwamba kuna sherehe ya birthday.

“Welcome home Eddy and Cauther”

Nilisoma maandishi yaliyo andikwa kwenye moja ya pambo.

“Suprize”

Tukastuka kidogo mara baada ya wana familia ya Cauther wakiongozwa na Judy wakishuka ngazi za gorofani huku wakiwa wamebeba keki kubwa.

“Aha bado kidogo nikimbie”

Nilizunguza kwa utani na kuwafanya watu wacheke. Tukaanza kukumbatiana nao huku tukusalimiana.

“Sasa mwanangu uta pumzika”

Mama mkwe alizungumza huku akiwa amenikumbatia.

“Ni kweli mama”

“Karibu sana nyumbani”

“Nashukuru sana mama yangu”

“Ohoo mjukuu wangu amekuwa mrembo sasa”

“Hahaa ni kweli, amekuwa mrembo mrembo. Mama kija nakuona”

Nilimtania Judy na tumbo lake kwani limesha kuwa kubwa.

“Jamani kaka”

“Njoo nikukumbatie”

Nikakumbatiana na Judy kisha tukaachiana.

“Una jisikiaje?”

“Nipo poa kabisa sasa hivi nina nguvu za kutosha tofauti na pale awali nilikuwa ni mtu wa kulegalega.”

“Hahaa ni hali”

“Wifi nakuona kwenye ubora wako”

Cauther alizungumza hukuw akikumbatiana na Judy.

“Yaani natamani sana kubeba mwanangu”

“Usijali Mungu ni mwema na wewe uta beba. Upo salama lakini”

“Namshukuru Mungu nipo salama salimini kabisa”

“Kaka nakuomba”

“Kabla hamjaondoka jamani zimeni mishumaa jamani ikiwa ishara ya kukaribia nyumbani”

Mama mkwe alizungumza, mimi na Cauther kwa pamoja tukazima mishumaa hii kwa kuipulizia na watu wote wakashangilia mama mkwe akatuvisha mataji kama mila zao za kiarabu zinavyo zungumza na akatupaka rangi fulani katika utosi wa mapaji yetu ya uso kisha mimi na Willy tukapandisha gorofani na tukaingia katika chumba cha kuongozea kamera zote za nyumba hii zipatazo mia moja na ishirini.

“Niambie kuna nini”

Willy akawasha moja ya computer na akanionyesha ramani ya eneo ambalo silifahamu kidogo.

“Ni nini?”

“Hili ndio eneo ambalo makamu wa raisi yule adui yetu amejificha je una hitaji tumshambulie kwa drones akafilie mbali”

“Lipo wapi hilo eneo?”

“Israel kwa yule raisi mpuuzi ndio amempatia hifadhi mpuuzi mwenzake.”

Willy akavuta video inayo rekodiwa kwa satelaite na tukaona gari nne nyeusi zinazo fanana zikiingia eneo hilo huku zikiwa na bendera ya Israel. Tukamuona makamu wa raisia kaitoka ndani ya nyumba moja akiwa ameongozana na mke wa raisi wa zamani. Tukamuona raisi wa Isreal akishuka kwenye gari ya tatu kutokea nyuma huku akiwa katika ulinzi mkali. Nikashusha pumzi nyingi kwani maadui zangu wamekutana sehemu moja na hakuna haja ya kuwaacha hai zaidi ya kuwaangamiza tu



Kabla sijazungumza chochote mlango wa chumba hichi ukafunguliwa, Cauther akaingia ndani hapa.

“Vipi mboan mumetukimbia?”

Cauther alizungumza huku akitazama tv inayo munyesha makamu wa raisi, raisi wa Israel, pamoja mke wa aliye kuwa raisi wa Tanzania.

“Hawa nao vipi mume wangu?”

“Hao ni maadui zangu, ambao walinitesa sana kipindi nipo raisi, walitumia uadui wetu kuwadhuru walisio na hatia”

“Sasa hapa imekuwaje muna waona?”

Swali la Cauther likatuafanya mimi na Willy kutazamana.

“Ahaa mke wangu, hapa tupo mubashara kabisa nah ii ni video inayo rekodiwa kwa Satelaite. Unacho kiona hapa ndio kinacho endelea. Tunacho kihitaji hivi sasa ni kufanya shambulizi la kumuua huyu mshenzi”

“Mmmm ila mume wangu huoni kwamba ni hatari, usilipe ubaya kwa ubaya. Umesha toka madarakani sasa hivi tena kwa amani kabisa. Achana na maswala ya visasi kwa maana wakijua wewe ndio muhusika basi wana weza kulipitaza kisasi kupitia sisi. Tafadhali mume wangu usije ukafanya hilo jambo nakuomba”

Mke wangu alizungumza kwa sauti ya upole na kunifanya nishushe pumzi nyingi huku nikimtazama.

“Willy ongea bwana na kaka yako. Maswala ya uadui sio mazuri”

“Nimekuelewa shemeji”

“Sawa mimi nipo sebleni, tuna wasubiria sherehe ianze”

“Sawa tuna kuja”

Cauther akatoka ndani hapa, nikakaa kwenye moja ya kiti.

“Vipi kaka?”

Willy aliniuliza huku akinitazama machoni mwangu. Tukaona kundi la watoto wakitoka ndani ya nyuma hii kubwa na wakaanza kusalimiana na raisi wa Israel.

“Aise tungefanya shambulizi tungeua watoto wasio na hatia”

Nilihamaki kwa maana hata kwenye vita kuua watoto wadogo ni jambo lisilo kubalika japo vita za miaka ya sasa hazinaga macho.

“Aisee ni kweli, je tusitishe?”

“Sitisha tuachane nao kwa sasa ila ina bidi uwe nao macho mara kwa mara”

“Sawa kaka, vipi ule mpango wako kwa kwenda kuishi India bado upo?”

“Mmm upo ila nita kaa kaa hapa kwa miezi kadhaa kisha nitaondoka zangu. Nina mpango wa kwenda nyumbani”

“Nyumbani, nyumbani ni wapi kwa maana toka nimekujua hujawahi kuniambia nyumbani ni wapi?”

“Makete, kwenye kile kituo cha watoto yatima ndio nyumbani kwetu. Kabla ya kwenda ina bidi mwanangu akapajue sehemu ambayo nimetokea”

“Hahaha kaka sasa Nadia na udogo huo ata elewa nini?”

“Kuna kupiga picha, hata tukiwa mbali huko siku akija kukua, picha zitamueleza ni wapi alipo tokea”

“Hapo nimekuelewa kaka. So ni nilini una kwenda na mimi niunge tela kwa maaa nimechoka kukaa Dar”

“Mama K atakuruhusu uende?”

“Aha sasa hivi amani ipo vizuri. Ata niruhusu ila sijui sina uhakika sana kwa maana ni hamsini kwa hamsini”

“Sawa bwana. Twende tukasherekee”

Tukatoka ndani hapa na tukajumuika na wana familia huku Sudy akiwa ndio mchoma nyama mkuu wa sherehe hii.

“Ehee niambie Sudy ule mpango walo ulikwendaje?”

“Namshukuru sana Mungu kaka, shemeji aliweza kuniunga mkono hadi nimefungua sehemu yangu nzuri na ya kisasa”

“Ila wateja si wanakuja?”

“Nashukuru Mungu wana kuja wengi sana. Wale wapemba wezangu wana nichukia sijui kwa nini?”

“Nisikilize Sudy mdogo wangu. Kwenye haya maisha kama una kuwa na boss ambaye ana kutegemea kwenye kuendesha biashara yake na wateja wana kuja kwa ajili yako. Siku utajapo ondoka tambua hii timu kubwa ya watu ulio kuwa nayo nyuma uta ondoka nayo. Na ukisha ondoka nayo ni lazima ata kuchukia tu kwa sababu sisi binadamu sio watu tuna penda maendeleo ya mtu mmoja mmoja.”

“Ila kweli kaka, yaani sasa hivi wana hadi kuniroga”

“Weee”

“Haki ya Mungu kaka, yaani nina tumiwa mauza uza ya ajabu. Kama ningekuwa sija niweka vizuri siku nyingi sana ndugu yako ningekuwa nimesha potea”

“Pole sana, ndio upambane sasa, kwa maana una jua tulipo tokea, toka nimekuwa dereva taksi hadi leo hii raisi mstafu umekuwa ni kijana ambaye umeniheshimu mimi na mke wangu”

Nilizungumza huku nikila mshikaki ulio chomwa vizuri na Sudy.

“Una jua kaka, heshima ni jambo ambalo nilikubwa na wazazi wangu. Kama ningekuwa ni mtu wa kujikwenza haki ya Mungu ikulu nisinge ingia na ningeisikia kwenye bomba”

“Hahaha sasa sikia Sudy. Kuna swala nahitaji kukushirikisha”

“Swala gani kaka?”

“Baada ya miezi kadhaa hivi nita kwenda kuishi India mimi na familia yangu. Maisha yetu tuta yahamishia huko na Tanzania tuta kuwa tuna kuja kutembea tu. Kitu ambacho mimi na mke wangu tulikifikiria ni kufungua mgahawa mkubwa ambao utakuwa una uza vyakula ya kiafrika zaidi. Hivyo mgahawa utakapo kamilika nita kuomba uje kuungana na sisi uwe mpishi wa hizi mambo kwa maana hichi ni kipaji chako kuchoma nyama”

“Mimi sina neno kaka, yaani hata ukisema sasa hivi mimi nipo tayari kukufwata kaka popote uendapo”

“Nashukuru sana ndugu”

“Shem”

Nadia aliniita huku akitufwata eneno hili tulilo simama huku Sudy akiendelea kuchoma nyama hii.

“Niambie mke mdogo”

“Safi tuna weza kuzungumza”

“Bilas haka”

Tukasogea pembeni kidogo eneo ambalo sio rahisi kwa mtu kusikia tunacho kizungumza.

“Niambie”

“Eddy kusema kweli nina nyeg* hapa nilipo najisikia hadi kuumwa. Tafadhali naomba ukanikune”

“Aisee na watu wote hawa. Familia yako ipo hapa, tuna anzaje kufanya mapenzi”

“Si tuna aga kwamba tuna kwenda sehemu kununua vitu?”

“Nadia sasa hivi mimi sio kama yule Eddy wa zamani kwamba nina weza kuendesha gari nikiwa peke yangu na kwenda sehemu yoyote nitakayo. Mimi sasa hivi ni raisi mstafu, nikitoka nina toka na wale wavaa suti nyeusi una waona kule. Ndio maana ina kuwa ngumu”

“Nihurumie baby, nina nyeg* haki ya Mungu, yaani toka siku ile unitomb** ofisini kwako hadi leo sijawahi kutomb** please baby”

Nadia alizungumza kwa sauti ya ushawishi hadi jogoo wangu akaanza kunyanyuka nyanyuka katika suruali yangu.

“Sawa acha niandae mazingira kwa maana hii ni nyumba yangu hivyo nita jua wapi kwa kukupeleka”

“Poa usinicheleweshe yaani nina weza kumparamia hata mtu yaani si kwa nyege hizi”

“Usifanye ujinga usije ukapigwa makofi saa hizi ukaharibia watu sherehe”

“Usijali shem hakuna wa kunipiga”

“Alafu umekunywa ehee?”

“Nimekunywa glasi moja ya wyne”

“Okay usikae mbali na simu yako”

“Sawa shemeji”

Nadia akaondoka na nikarudi eneo alipo simama Sudy.

“Huyu mtoto nina mpenda sana”

Sudy alizungumza huku akimtazama Nadia jinsi anavyo tembea kuelekea ndani.

“Huja mtongoza hadi leo?”

“Ahaa namuogopa balaa”

“Kwa nini una muogopa”

“Una jua huyu hajazoea zoea watu kama ilivyo kwa dada yake”

“Sasa wanawake kama hawa ndio walaini, wenyewe tuna waita maharage maji mara moja”

“Ahaa kaka kuna siku nilijaribu kumgusia tu weeee, nilujuta alinichama balaa”

Tukajikuta tukicheka kwa nguvu hadi watu walio simama karibu nasi wakageuka na kutuangalia.

“Kumbe watoto wa kiarabu wana ongea sana, yaani cha kumsuhukuru Mungu nilikuwa mimi na yeye na kwenye gari pia akanishusha”

“Hahahahaha sasa mulikuwa muna kwenda wapi?”

“Kipindi tuna fungua ule mgahawa kuna pesa tulikuwa tuna kwenda kuitoa benki ili tulipe mafundi, dada yake alimuagiza. Sasa tumesha toa pesa tuna rudi kwenye mgahawa ndio nikaanza swaga zangu za kutongoza aisee kaka wewe sikia tu. Nilichambwa, hadi nikashushwa kwenye gari yaani nilipanda bajaji kurudi kwenye mgahawa ndio maana hadi leo hanisemeshi wala kunisalimia”

“Aise pole sana best”

“Nashukuuru kaka yaani sio mchezo”

“Nawaona wenyewe”

Mama mkwe alizungumza huku akitabasamu.

“Karibu mama yangu”

“Nashukuru, kijana una choma nyama vizuri aisee. Nikipata maharusi nitakuwa nina kuchukua”

“Nashukuru sana mama yangu”

“Eddy mwanangu”

“Ndio mama”

“Naona sasa mambo yamekwisha mwanangu”

“Ni kweli mama yamekwisha kwa kiasi fulani”

“Sasa mwangu, mpamgo wa kuonana na baba yako una uwaje kwa maana jamani na mimi nime mmiss”

“Usijali mama tuta fanya utaratibu wa wewe kuja kuishi nasi huku. Na nina ombi moja mama”

Nilizungumza huku nikimshika mkono mama mkwe na tukasimama pembeni.

“Ndio mwanangu”

“Ninge omba pale baba atakapo rudi basi muje kuishi nasi hapa nyumbani. Ona hili jumba lililvyo kubwa na hatuna wa kuishi naye zaidi ya Nadia mkubwa na mdogo”

“Mimi sina tatizo baba yangu ila sijajua kama baba yako ata kubali”

“Hilo niachie mimi mama wala usijali”

“Sawa baba yangu mwneyezi Mungu akibariki”

“Ame”

Mama mkwe akaondoka eneo hili na nikerudi eneo alopo Sudy. Tukaendelea kusaidia kuchoma nyuma hii. Majira ya saa moja kasora nikaingia eneo ambalo lipo chini ya ardhi na milango yake ina funguliwa kwa kutimia fingerprint ya vidole vyangu au vya mke wangu. Nikakagua mazingira ya eneo hili, kisha nikatoa simu yangu mfukoni na kuitafuta namba ya Nadia. Nikatamani kumpigia ila nafsi yangu ikasita kidogo.

‘Tamaa ya siku moja isije ikavunja ndoa yangu’

Nilizungumza huku nikisitisha mpango huu kwani mazingira hayarushuu kabisa. Nikarudi eneo la juu na kuendelea kusherekea kustafu kwangu na wana ndugu. Muda ukazidi kusonga mbele na mtu mmoja baada ya mwengine akaelekea chumbani kulala kwa kuchoka.

“Mume wangu mimi na kwenda kulala”

Cauther alizungumza huku akikinyanyua kichwa chake mapajani mwangu kwa maama alikuwa amejilaza huku tukitazama filamu ya mapigano hapa sebleni pamoja an wana familia wengine.

“Ngoja nikusindikize”

(AIISSII YOU KILL ME CHAPTER FOUR(Killer) inazidi kusonga mbele. Wahi sasa ujiunge kwenye group WhatsApp 0657072588 kwa sh 4000/= tu.

Karibu sana)

Nadia akanikata jicho moja kali ila sikujali hilo. Tukapanda hadi gorofani, tukaingia chumbani na kumtazama vizuri mtoto wetu na kumkuta akiwa amelala.

“Nimechoka mume wangu”

“Vipi huna hamu na mimi”

“Ninayo mume wangu ila kwa leo nakuomba nipumzike, nakuahidi asubuhi nitakupa. Samahani lakini mume wangu”

“Usijali najua umechoka mke wangu leo mishemishe zilikuwa nyingi”

“Ni kweli baby”


ITAENDELEA


0 comments:

Post a Comment

BLOG