Search This Blog

Wednesday, November 18, 2020

MKE WA RAISI (PRESIDENT‘S WIFE) SEHEMU YA 2/10

 

 


 MKE WA RAISI (PRESIDENT‘S WIFE)

WRITER…………………………………………EDDAZARIA G.MSULWA
WEBSITE………………………………………… www.storyzaeddytz.com
CONTACT……………………………………….. 0657072588/0768516188
AGE……………..18+ 

SEHEMU YA 2 KATI YA 10

 


Ofisi nzima watu wakaka kimya huku macho yao wakimtazama jeneral wa jeshi aliye pewa amri ya kuanda amakombora ikiwa ni amri kutoka kwa raisi Dustan.

“Muheshimiwa raisi haya maamuzi hayo uliyo yachukua ni magumu sana”

Silvester alizungumza huku akimtazama raisi Dustan anaye onyesha dhairi kwamba maamuzi aliyo yachukua ni maamuzi aliyo yachukua ni kutokana na hasira aliyo kuwa nayo.

“General hii ni amri fanya kama ninavyo kuambia sawa”

“Sawa muheshimi raisi”

***

Adrus akafanikiwa kufika ofisini kwa makamu wa raisi, akaruhusiwa kuingia ndani ya ofisini, akamtaka Eddy akiwa amekaa kwenye sofa pamoja na Shamsa.

“Karibu Adrus”

Eddy alizungumza huku akimuonyesha Adrus sehemu ya kukaa.

“Shukrani muheshimiwa”

Adrus akaka kwenye sofa huku akiweka sawa koti lake la suti.

“Unaendeleaje?”

“Nipo sawa muheshimiwa raisi”

“Pole tatizo ni nini hadi ukapoteza fahamu”

Adrus hakuhitaji kuzungumza, akatoa simu yake mfukoni na akaiweka video inayo onyesha shambulizi lililo fanywa nchini Marekani huku Naomi akionekana jinsi anavyo shambuliwa kwa kupigwa risasi kadhaa kifuani mwake.

“Huyo msichana unaye muona hapo aliye pigwa risasi hapo ni mpenzi wangu”

“Aissee pole sana, kwa hii hali sidhani kama upo sawa, ni vyema nikakupa muda wa kupumzika”

“Hapana makamu wa raisi nipatie tu kazi, ninahitaji kuifanya hii kazi ambayo umeniambia”

“Oparesheni imebadilika”

Eddy alizungumza huku akimtazama Shamsa aliye kaa kimya, akiwaza ni jinsi gani anavyo weza kumpata mwanaye.

“Imebadilika kivipi mkuu?”

“Mwanangu na mdogo wangu wametekwa, na watekaji ni watu ambao nina wafahamu na wananifahamu mimi vizuri sana”

“Wapo ndani ya nchi hii?”

“Hapana wapo nje ya hii nchi, hadi sasa hivi sijafahamu ni wapi walipo ila tukifahamu ni wapi walipo ila….”

“Eddy hawa si D.F.E?”

Shamsa alizungumza huku akimtazama Eddy

“Ndio”

“Ile Laptop ya mzee Godwin ipo wapi?”

Shamsa alizungumza huku akisimama kwenye sofa alilo kalia

“Ipo nyumbani”

“Inabidi nikaichukue sasa hivi”

“Usiende nyumbani sasa hivi”

“Eddy mtoto wetu amatwekwa, hili halikuuingii akili au?”

Shamsa alizungumza kwa ukali hadi sura yake nzuri ikiwa imebadilika kabisa.

“Kumbuka kwamba Phidaya hatakiwa kufahamu hili swala”

“Eddy hujui uchungu nilio nao, hujui jinsi gani roho yangu inavyo niuma. Phidaya naye anauchungu kwa wanae anao watoa tumboni mwake sawa”

Shamsa akaanza kutembea kuelekea mlangoni, Eddy kwa haraka akasimama na kumuwahi kumshika mkono na kumfanya Adrus abaki akishangaa kwani hatambui ni mahusiano gani yanayo endelea katika ya Shamsa na makamu wa raisi.

“Shamsa tuliza kichwa chako hembu kuwa na heshima basi tambua unazungumza mambo ambayo watu wengine hawastahili kusikia”

“Nani, Adrus hastahili kusikia. Adrus sikia, mimi na Eddy tuna mtoto wetu anaitwa Junio Jr, haya sasa amesha jua kuna jengine jipya ambalo unahitaji kuzungumza?”

Shamsa alizungumza kwa sauti ya juu huku akimtazama Adrus.

“Eddy namuhitaji mwanangu, namtaka mwanangu”

Shamsa akaanza kulia upya huku akimpiga piga Eddy kifuani mwake, taratibu Eddy akamkumbatia Shamsa huku akijitahidi kuishika mikono yake kwa nguvu.

“Atarudi mtoto wetu sawa”

Eddy alizungumz ahuku akishindwa kabisa kuyazuia machozi yake.

“Lini Eddy, lini atapatikana”

“Nakuahidi atapatikana, jikaze Shamsa, tuendelee kufanya mambo mengi”

Taratibu Shamsa akamuachia Eddy na kurudi katika sofa huku akijikunyata kwa kukosa furaha.

“Muheshimiwa makamu wa raisi hili ni swala la kiserikali kwa manaa aliye tekwa hapo ni mwanao unaonaje tukashirikisha viongozi wa usalama”

“Hapana Adrus, hili swala sihitaji mke wangu kulifahamu, ndio mana anikakuchagua wewe ili ulisimamie hili swala”

“Inabidi hapo muheshimiwa tuweze kufahamu sehemu walipo. Ila hao watekaji wamezungumza kitu gani?”

“Wamenipa sharti la kumuachia mke wangu ili wanipe mtoto na mdogo wangu”

“Mmmmm”

Adrus aliguna huku akishusha pumzi nyingi sana

“Waliwapigia simu?”

“Ndio”

“Hembu hiyo namba”

Shamsa kwa haraka akamkabidhi Adrus simu yake ya mkononi. Adrus akaitazama namba iliyo piga muda mchache ulio pita.

“Hii namba inatoka nchini Uingereza kitu ambacho tunaweza kukifanya hapa ni kutafuta mtu wa IT, mwenye uwezo wa kuitafuta hii namba ni wapi ilipo na itasaidia kwa sisi kuweza kulifahamu hilo eneo na kama itawezekana basi niweze kwenda kulishuhulikia hili tatizo haraka iwezekanavyo”

“Sawa, hapa ofisini kwangu kuna watu wa IT”

“Basi tumpate mmoja ambaye tutaweza kumuamini kwa maana hii kazi muheshimiwa unaipeleleka kifamilia zaidi”

“Sawa”

Kwa haraka Eddy akatembea hadi mezani kwake, akanyanyua mkonga wa simu ya mezani na kumpigia sekretari wake.

“Njoo ofisini kwangu”

“Sawa mkuu”

Eddy akairudisha mkonga wa simu yake mezani na kumsubiria sekretari huyo ambaye hakumaliza hata dakika mbili akaingia ofisini humu.

“Judy unamfahamu mtu ambaye anaweza kushuhulika na maswala ya IT humu ofisini?”

“Ndio muheshimiwa yupo Ludovic anaweza kushuhulika katika hilo swala”

“Muite sasa hivi muambie kwamba aje na vifaa vyake”

“Sawa mkuu”

Judy akatoka ofisini humu kwa Eddy.

“Muheshimiwa ninakuomba uweze kunisaidia katika hili swala lililo jitokeza nataka kudhibitisha kwamba mpenzi wangu yupo hai au amefariki”

“Sawa, ngoja nilifanye kwa sasa”

Eddy akatoa simu yake mfukoni na kumpigia balozi wa Tanzania, nchini Marekani, simu ikaita kwa muda kiha sikapokelewa.

“Habari yako mzee Lusonge”

“Salama habari yako makamo wa raisi”

“Salama, kuna tukio la shambulizi limetokea huko Marekani jana, sasa kuna mtu ninahitaji ufwatilie kama yupo hai au amefariki”

“Anaitwa nani?”

Eddy akamtazama Adrus na kwa ishara ya mdomo akamuuliza Adrus aliye mtajia haraka jina la Naomi.

“Naomi”

“Sawa muheshimiwa usikate simu niwasiliane na Gavarna wa jimbo lililo tokea tatizo”

“Sawa”

Eddy akasubiria kwa dakika kadhaa, kisha bwana Lusonge akarudi hewani.

“Muheshimiwa makamu wa raisi, muhusika wa jina hilo alikuwa ni mlinzi wa mtoto wa raisi Dustan?”

“Yaa alikuwa mlinzi”

“Habari nzuri ni kwamba yupo hai, ila hali yake bado ni mbaya yupo chumba cha kuuguza wagongwa mahututi”

Eddy ili kumpa matumaini Adrus ili aifanye kazi iliyopo mbeleni mwao vizuri, akaiweka simu yake loudspeaker kisha akamuomba bwana Lusonge kurudia alicho kizungumza.

“Naomi yupo hai, ila yupo katika chumba cha wagongwa mahututi hali yake sio nzuri sana”

“Nashukuru sana bwana Lusonge”

“Nashukuru pia”

“Ila ninakuomba uwe unanipa taarifa ya kila hali ambayo itakuwa inaendelea kwa binti huyo”

“Sawa muheshimiwa”

Eddy akakata simu na kumtazama Adrus aliye ikunja mikono yake kama wanavyo sali katika imani yake ya kiislam, akaanza kumuomba Mungu ammjalie mpenzi wake afya njema na kumuepusha na kifo kilichopo mbele yake. Adrus akafumgua macho yake na kumtazama makamu wa raisi.

“Mungu atamsaidia atapona”

“Inshallah”

Akaingia Ludovick huku akiwa ameshika laptop yake mkononi.

“Samahani muheshimiwa kwa kuchelewa kufika”

“Usijali kuna kazi ninahitaji uifanye sasa hivi”

“Kazi gani?”

“Hii hapa”

***

“John ila umesahau kuwapa muda wa kumtoa Phidaya”

Dokta Ranjiti alizungumza huku akimtazama John mara baada ya kukata simu.

“Usijali ninamjua Eddy, huwa hachelewi kutoa maamuzi yake”

“Ila kumbuka huyo tuloye muomba ni mke wake”

“Wewe kuwa mshabiki, kila kitu nitakifanya mimi”

John akafungua simu yake na kuitoa laini aliyo itumia kumpigia Eddy.

“Mbona unaivunja laini?”

“Wewe ni dokta na mimi nimekua katika harakati hizi kwa mika ishirini kwa sasa, ni lazima Eddy atatumia satelaiti kujua ni wapi nilipo na akijua, dunia nzima itatugeukia na itakuwa ni tatizo kubwa jengine ambalo katika uongozi wangu kwa sasa sihitaji liwepo”

“Hapo nimekuelewa mkuu”

“Nyinyi washenzi nikitoka hapa ninawaambia nitawakata vichwa vyenu”

Sa Yoo alizungumza kwa hasira huku ajititahidi kujitoa kwenye kamba hizi alizo fungwa.

“Hahaaaa”

Jonh alizungumza kwa dharau huku wakitoka katika chumba hichi huku akiwa amembeba Junio Jr na kutoka ndani humu.

“Kimbery hakikisha vijana wako wanamlinda huyu haraka iwezekanavyo”

“Sawa mkuu”

“Huyu kijana nitakuwa naye, sasa sijui anakula chakula gani?”

“Nitajaribu kumuandalika vyakula ambavyo watoto wanapenda”

“Sawa utakuja kule kwenye nyumba yangu”

“Sawa mkuu”

John na dokta Ranjiti wakaingia kwenye gari na kuondoka na kumuacha Kimbery akielekea katika nyumba anayo ishi katika kisiwa cha hapa msituni.

***

Mashine zinazo msaidia Naomi katika kuyapa mapafu yake hewa yanaendelea kufanya kazi taratibu, huku madakari wakiwa bado hawana matumaini ya kupona kwake.

“Ni binti mzuri sana”

Daktari mmoja alizungumza huku akimtazama Naomi usoni mwake.

“Yaa ni mzuri sana Mungu amsaidie”

“Sawa, ila ni kwa nni Gavana amemuulizia huyu binti?”

“Kusema kweli sifahamu, hata mimi na wewe ni kitu kimoja”

Daktari huyu akashika kitasa cha mlango wa chumba hichi alipo Naomi, kitendo cha kufungua mlango akasuhudia wanajeshi wawili wakianguka chini huku kundi la watu walio funika nyuso zao kwa vitambaa vyeusi huku mikononi mwao wakiwa wameshika bunduki wakija katika eneo la chumba hichi alicho lazwa Naomi, jambo lililo mfanya dokta huyu kufunga mlango kwa ndani huku mwili wake ukimtetemeka sana kwa woga.



“Kuna kitu gani kinacho endelea?”

“Shiiii hospitali imevamiwa”

Daktari alimjibu huku mwili mzima ukimtetemeka, wakamtazama Naomi aliye lala kitandani huku hatambui ni kitu gani kinacho endelea. Mlango wa chumba hichi ukaanza kubamizwa kwa nguvu jambo lililo wafanya madaktari kuchanganyikiwa, kwani hawajui wavamizi hawa wamefwata kitu gani katika hospitali hii. Kwa haraka huku wakisaidiana wakachukua kabati kubwa lililopo chumbani homo, wakalisogeza hadi mlangoni na kuligandamizi. Wavamizi walio tumwa kuja kuhakikisha kwamba wanamuangamiza Naomi, miongoni mwa wanajeshi walio wasababishia maafa nchini Pakistani. Madaktari wakazidi kuchanganyikiwa mara baada ya kuona risasi zikipigwa na kutoboa kabati hilo la mbao.

“Ehee Mungu tusaidie sisi?”

Daktari alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake.

***

Habari ya uvamizi wa hospitali ya jeshi ikafika ikulu, watui wote waliomo katika ukumbi wa mkutano wakijadili kuhusiana na ni jinsi gani watayatupa makombora yao ya kivita nchini Pakistani ili kulipiza kisasi cha magaidi ambao wamesababisha maafa makubwa katika moja ya gorofa la kiuchimi la twin tower, huku wakiwa wameua mamia ya vijana walio kuwa wameudhuria katika sherehe ya rafiki wa mtoto wa raisi Dustan.

“Imekuwaje wamevamia hospitali ya jeshi?”

Raisi Dustan alizungumza huku akitazama video ya satelaiti inayo onyesha jinsi wavamizi wao walivyo wengi na wamefanya shambulizi la kustukiza kwa wanajeshi wanao linda hospitali hiyo.

“Muheshimiwa raisi wavamizi walio fika katika eneo hilo ni zaidi ya mia moja, na wengi wamefika kwa gia ya kuumwa na kudai kwamba ni wagonjwa”

“Ninaamuru wauwawe wote. Ilowezekana muwakamate ili waweze kutaja ni wapi wezao walipo, sawa mkuu wa jeshi”

“Ndio muheshimiwa raisi”

Mkuu wa jeshi kwa haraka akapiga simu kwa kitengo maalumu cha makomandoo, walio funzu mafunzo ya juu sana ya kupambana na mashambulizi ya kigaidi. Kisosi hicho cha watu kumi kwa haraka kikaingia ndani ya helicopter na kuianza safari ambayo haikuchukua hata dakika kumi na tano, wakawa wamefika katika hospitali hii ya jeshi ambayo magaidi wengi wameivamia na kua asilimia kubwa ya wanajeshi ambao hawakuelewa ni kitu gani kinacho endelea.

Makomandoo hawa wakajigawa katika vikundi vya watu wawili wawili na kutawanyika katika hospitali hii kubwa, kutokana wamepewa amri ya kuu, kila waliye muhisi kwamba ni gaidi wao walimpiga risasi na kufa, wakazidi kusonga mbele na kuzama zaidi ndani ya hii hospitali ambayo wahudumu pamoja na baadhi ya wagonjwa wameshambuliwa kwa kupigwa risasi nyingi sana.

“Ohooo Mungu wangu”

Mwanajeshi mmoja alizingumza baada ya kukuta mwanamke mmoja aliyekuwa akifanyiwa upasuaji, ili aweze kujifunga salama, amewawa huku mwanaye pamoja na madaktari wakiwa wamechinjwa kikatili sana. Bahati kwa siku ya leo haikuwepo kwa magaidi hawa ambao wanaendelea kung’ang’ana na mlango wa chumba alicho lazwa Naomi, japo wamajifunika sura zao na kuvaa majaketi ya kuzuia risasi, ila kwa jinsi walivyo shambuliwa na makombandoo hao walijikuta wakiteketea na kwa bahati nzuri wawili wakaamua kujisalimisha. Kwa haraka makomandoo hawa wakawakamata na kuwafunga pingu.

“General oparesheni imekwenda vizuri”

“Kazi nzuri vijana wangu, vipi kuna mlindi wa mtoto wa raisi, agent Naomi je yupo?”

“Ngoja tuendelee kuangalia katika chumba hichi ambacho walikuwa wana hangaika, nina imani kwamba atakuwepo”

“Sawa colony, hakikisha kwamba kila kitu kina kwenda sawa”

“Sawa jeneral”

Makomandoo wawili wakajaribu kuufungua mlango huu ulio jaa matundu ya risasi.

“Kama kuna mtu ndani fungua, sisi ni wanajeshi wa Marekani, tumekua kutoa msaada”

Sauti ya mwanaume huyu ikawafanya madaktari hawa walio kuwa amejificha chooni kuchungulia mlangoni kwani tayari walisha kata tamaa na kuamini kwamba leo ndio siku yao ya mwisho kuishi hapa duniani.

“Tutawaamini vipi?”

Daktari mmoja alizungumza.

“Hichi ni kitambulisho changu kinacho onyesha kwamba mimi ninaye zungumza ni kiongozi wa kikosi hichi cha jeshi la Marekani”

Colony Dismas, alizungumza huku akiingia kitambilisho chake katika shimo moja kubwa la lililo tobolewa kwa risasi, daktari akajikaza hadi kilipo angukia kitambulisho, akakiokota na kukitazama kwa muda.

“Umeamini?”

Daktari huyu alishindwa kujibu kabisa, mwanaze alipo jikaza na kufika mlangoni hapo naye akakisoma kitambulosho hicho walicho kishika.

“Mumeamini?”

“Ndio tumeamini”

Madkatari hawa wakaanza kusaidiana kulisogeza kabati hilo, wanajeshi hao wakingia ndani ya chumba hicho, wakasalimiana na madaktari hawa wawili kisha wakamtazama Naomi.

“General Naomi hajaudhurika bado anaendelea kupumulia mashine”

“Colony hakikisha kwamba munamchukua Na kumleta hapa ikulu”

“Sawa muheshimiwa raisi”

“Je mumefanikiwa kuwakamata wangapi?”

“Wawili wamejisalimisha?”

“Ninawaomba muweze kuwafanyia uchunguzi wa kina na nina imani watatutajia ni sehemu gani ambayo wamejificha na kumficha mwanangu”

“Sawa muheshimiwa raisi”

***

Eddy akamuonyesha Ludovick namba ya John ambayo imetoka kuwapigia dakika kadhaa zilizo pita.

“Hiyo ni namba ya gaidi mmoja duniani amenipigia muda si mrefu, ninahitaji uhakikishe kwamba unaitafuta na kujua yupo wapi”

“Sawa muheshimiwa”

Ludovick alijibu huku akiitazama namba hii kwa umakini, akainakili na kuingiza katika laptop yake, akaanza kuitafuta namba hii kwa satelait. Kila jinsi alivyo jaribu kuitafuta hakuweza kuipata na namba inaonyesha kwamba haipo kabisa hewani.

“Vipi umempata?”

“Hapana muheshimiwa haipatikani”

Jibu la Ludovick likawa kama kisu kikali kilicho yakata matumaini ya Shamsa aliyokuwa ameyajenga kwa muda muda fulani akiamini kwamba kijana huyo anaweza kumpata John.

“Kwa nini hapatikani?”

Shamsa aliuliza kwa hasira hadi Ludovivk akastuka.

“Heee Shamsa tulia”

“Nitulie nini Eddy, kumbuka aliye potea hapa ni mtoto, mbona unakuwa mzito hivyo au ndio uongozi wako umekulevya?”

Kwa jicho kali na lililo jaa hasira alilo mtazama Shamsa likamfanya kila mtu ndani ya chumba hichi aamini kwamba kiongozi wao amekasirika sana na laiti wasinge kuwepo ndani ya chumba hichi basi Shamsa angezwabwa japo hata kofi moja zito.

“Dogo umeangalia vizuri na kujua kwa nini hapatikani?”

“Nina hisi ameivunja laini, kwa mana laingi ingekuwa ni nzima basi tungeweza kugundua ni wapi alipo”

“Shitiiiii”

“Mkuu unaonaje tukawaomba wana usalama nchini Uingereza wakatusaidia katika hili?”

Adrus alizungumza huku akimtazama Eddy usoni mwake kwa kujiamini.

“Hawawezi kutusaidia kwa lolote”

“Basi inabidi niende nchini humo ili nikafanye upelelezi wa chini kwa chini nina imani siku mbili zinanitosha kuhakikisha kwamba ninagundua ni wapi alipo tekwa mwanao”

“Sawa, sasa fanya hivi nenda nyumbani sasa hivi, jiandae, baada ya lisaa na nusu uwe hapa ninafanya mawasiliano kabisa na ubalozi wa Uingereza hapa nchini na wataidhinisha kwenda kwako kama mpelelezi sawa”

“Nimekuelewa muheshimiwa”

Adrus akatoka ofisini humu na moja kwa moja akatoka nje, akakodisha pikipiki na kuelekea nyumbani kwao.

“Dogo nenda kaendelee kuitafuta hiyo namba, likipatikana eneo husika ninakuomba uniambie”

“Sawa muheshimiwa makamu wa riasi.”

Ludovick akaanza kupiga hatua hadi mlangoni, akasimama kisha akageuka na kuanza kurudi alipo simama Eddy.

“Muheshimiwa hivi hao magaidi hawajakutumia japo video au sauti yoyote?”

“Video ipo hii hapa”

Eddy alizungumza huku akimuonyesha Ludovick video iliyopo katika simu ya Shamsa.

“Ok hii itanifa”

Ludovick kwa haraka akachomeka waya wa USB katika laptop yake kisha na kuuchomeka katika simu ya Shamsa, akaihamisha video hii.

“Muheshimiwa ngoja nikaitafute”

“Sawa fanya hivyo dogo hakikisha kwamba unaipata”

“Sawa”

Lodovick akaondoka katika eneo hili na kuwaacha Shamsa na Eddy walio tazamana kwa hasira sana kana kwamba mmoja wao ndio amehusika katika kumteka mtoto wao.

“Shamsa, siku nyingine sihitaji ujinga huu ulio ufanya ujitokeze mbele za watu”

“Ujijnga Eddy, kwahiyo kumdai mwanangu ni ujinga, unajua machungu niliyo pata kipindi nina jifungua, unajua?”

Shamsa alizidi kuzungumza kwa hasira huku akimsogelea Eddy, aliye jikita akurusha kofi ila kama Mungu alikuwa pamoja na Shamsa aliweza kuliona na kulikwepa.

“Eddy unataka kunipiga kisa mtoto wetu eheee?”

Shamsa alizungumza kwa sauti ya upole huku akilia kwa uchungu sana, sauti hiyo ikaanza kumfanya Eddy ajione ni muonevu kwani anacho kizungumza Shamsa ni kitu cha ukweli na kama ni mtoto amemshuhudia vizuri na amefanana naye kabisa.

“Am sorry”

Eddy alizungumza huku akijaribu kumshika Shamsa mkono wake wa kulia ila Shamsa akakataa kabisa kushikwa na kurudi kukaa kwenye sofa huku akilia, weupe wa Shamsa umebadilika kabisa na amekuwa mwekundu kwa kiasi fulani, nywele zake ndefu alizo kuwa amezibana vizuri zimechanguka kabisa. Eddy akamtazama kwa muda Shamsa, kisha akainyanyua mkonga wa simu yake mezani na kumpigia sekretari wake.

“Njoo ofisini”

Ndani ya dakika moja sekretari akaingia ofisini, kwa jinsi alivyo mtazama bosi wake na binti huyu akagundua fika kwamba ndani ya hii ofisi hali si shwari kabisa.

“Leo kuna vikao vingapi?”

“Una kikao waziri wa elimu, pia una kikoa na wafanya biashara wote hapa Dar es Salaam”

“Futa vikao vyote na uvisogeze hadi kesho”

“Muheshimiwa makamu wa raisi ila kumbuka hivi ni vikao muhimu sana na kuna baadhi ya wafanya biashara wamesha fika”

“Muembie muwakilishi wangu akaniwakilishe”

“Sawa muheshimiwa”

“Ila yoyote ambaye atahitaji kuonana na mimi muambie muheshimiwa ana dharura”

“Sawa muheshimiwa”

“Watu ambao unatakiwa kuwaruhusu kuingia ofisini kwangu ni hawa vijana wawili walio toka humu ndani umenielewa?”

“Ndio nimekuelewa”

“Alafu wasiliana na ubalozi wa Uingereza hapa nchini Tanzania, waeleze kuna mpelelezi kutoka ofisini kwangu atalekea katika nchi yao. Watoe visa pia mkatie tiketi kwa ndege inayo ondoka hapa Baada ya masaa mawili?”

“Sawa mkuu. Ila anaitwa nani?”

“Nani….Adrus”

“Sawa”

Kwa ishara ya mkono Eddy akamruhusu sekretari wake kutoka, Eddy akatembea hadi mlangoni na kuufunga mlango wa ofisi yake kwa ndani na kulisogelea sofa alilo kaa Shamsa anaye endelea kububujikwa na machozi, akamtazama kwa sekunde kadha huku akitamani kumshika japo mkono wake ila akajikuta akijawa na wasiwasi kwani tangu kumfahamu kwake Shamsa hajawahi kumuona akiwa katika hasira kama hii,

***

“John unajua ukihitaji kumshinda adui ni lazima umgombanishe na watu wake wa karibu”

Dokta Ranjiti alizungumza huku wakika ndani ya gari.

“Kivipi?”

“Hapa nimefikiria niitafute namba ya Phidaya”

“Eheee?”

“Nikisha ipata namba ya Phidaya, ninamtumia picha za huyu mtoto”

“Ukisha mtumia?”

“Hapo ni lazima Phidaya atachanganyikiwa na nitamuambia kitu kimoja kama anahitaji kufahamu ukweli wa hili jambo basi aonane na mimi”

“Hivi una akili kweli wewe, unahisi kwamba kumtumia picha inaweza kusaidia kumpata, haya kwa mfano akamuonyesha picha hizo mume wake utaonana naye vipi?”

“Usijali hilo swala niachie mimi”

“Ranjiti ranji kumbuka haudili na muuza mchicha au maharage, unadili na mke wa makamu wa raisi, unalielewa hilo wewe?”

“Ndio ninakuelewa wala usiwe na shaka”

“Sawa ninakuachia wewe tu hilo jambo”

“Sawa, ila nitahitaji vijana japo wawili watakao nilinda na nitaongozana nao hadi nchini Tanzania”

“Hahahaa, haya bwana kaka utachagua mwenyewe”

“Sawa”

Wakafika katika nyumba anayo ishi John, dokta Ranjiti akaanza kumpiga picha Junion Jr, alipo ridhika kwa wingi wa picha alizo mpiga mtoto huyu akaondoka katika eneo hili na kuelekea kwake, akakusanya nguo zake baadhi pamoja na kiasi kikubwa cha pesa, akawachagua vijana wake wawili ambao watamlinda, ili asiweze kujulikana kirahi akaondoka na ndege yake binafsi na lengo ni kutua nchini Kenya na Tanzania ataingia kwa njia ya gari.

***

“Mama mama”

Adrus aliita huku akitazama eneo la jikoni ila hakumuona mama yeka, akagonga mlango wa chumba cha mama yake ila hakuweza kusikia jibu la ina yoyote, ikamlazimu kuufunga mlango huo, akachungulia ndani ila hakumuona mama yeke. Aakitoa simu yake mfukoni na kumpigia mama yeke, simu ya mama yake ikaanza kuita kwa muda hadi ikakata. Hakuona haja ya kumpigia tena kwa manaa anatambua kwamba mama yake ni mtu wa mishe mishe hapa mjini na ana biashara zake ambazo huwa muda wa asubuhi huwa anazifwatilia.

Adrus akiangia chumbani kwake na kuanza kuingiza nguo zake katika begi lake dogo la mgongoni, akachukua hati yake ya kusafiria akaitazama kwa muda kisha akatabasamu akiamini kwamba hii ni mara yake ya pili anarudi nchini Uingereza na safari hii ni kwa kazi maalumu. Simu yake mfukoni ikaita kwa haraka akaitoa na kukuta ni mama yake ndio anaye mpigia, akaipokea na kuiweka sikioni.

“Mama?”

“Vipi nimekuta missed call yako?”

“Upo wapi?”

“Nipo Kariakoo, kuna vitenge nimekuja kuvichukua”

“Mama ninakwenda Uingereza”

“Uingereza si Marekani tena?”

“Ndio ni Uingereza hapa nipo nyumbani nimekuja kuchukua nguo baadhi, na ninatakiwa kurudi ofisini hivi sasa hivi”

“Ohooo na haya mafoleni, Mungu wangu kweli nitakuwahi mwanangu?”

“Ndio hapo mama”

“Daaa sasa inakuwaje?”

“Kwani upo Kariakoo eneo gani?”

“Nipo hapa Sheli ya bigbone ila ndio ninaelekea kwenye hayo maduka”

“Ngoja ninakodisha pikipiki, nikifika hapo Kariakoo utaniambia ni wapi ulipo, siwezi kuondoka pasipo kukuaga mama yangu”

“Sawa fanya hivyo nitaingia dukani mara moja, ukifika unipigie”

“Sawa na wewe usiweke simu kwenye pochi inaita hadi inakata”

“Ahaaa nisije nikaporwa buru, nitaiweka kwenye mkoba ila ukipiga nitaweza kujua”

“Sawa”

Kwa haraka Adrus akaingia simu yake mfukoni, akafunga chumbani kwake, akatoka nje ya nyumba yao na kuanza kutazama ni wapi kwa kuelekea ili aweze kupata dereva pikipiki atakaye mpeleka Kariakoo haraka. Gafla gari mbili aina ya benzi zenye rangi nyeusi, zikasimama mbele yake wakashuka watu nane walio valia suti nyeusi huku wakiwa wameshika bastoka zao, wakatoa vitambulisho vyao vinavyo onyesha kwamba ni walinzi wa raisi.

“Adrus Malidin, upo chini ya ulinzi kuanzia hivi sasa”

Kauli ya mmoja ya walinzi hawa ikamstua sana Adrus na kujikuta akipata kigugumizi hata cha kutembea kwa mana hatambui ni kosa gani ambalo amelifanya hadi kukamatwa na walinzi wa raisi Rahab.



“Kwa nini muna nikamata?”

“Utakwenda kujua mbele ya safari”

Adrus hakuwa na kipingamizi, akaingia ndani ya gari alilo elekezwa kuingia, walinzi wengine wakaingia kwenye gari walizo kuja nazo na kuondoka nyumbani hapa. Adrus akatoa simu yake mfukoni akataka kuwasilaiana na mama yake ila mmoja wao akachukua simu hiyo.

“Huruhusiwi kuwasiliana na mtu wa aina yoyote kuanzia hivi sasa”

“Kwa nini, ninahitaji kumpigia mama yangu, mumenikamata pasipo kosa lolote nimekubali pia kuongea na mama yangu?”

“Adrus fwata sheria”

“Siwezi kufwata sheria zipi, ikiwa mimi na nyinyi ni tofauti kumbukeni hilo”

Mlimzi aliye kaa siti ya mbele pembeni mwa dereva akamruhusu mwenzake kumpatia Adrus simu yake. Adrus kwa haraka akampigia mama yake.

“Eheee umefika wapi?”

“Mama ninaelekea ikulu nimekuja kuchukuliwa nyumbani, sinto weza kuja huko ulipo”

“Mmmm ndio unaondoka hivyo?”

“Nitakujulisha mama”

“Sawa utaipigia”

“Sawa mama”

Adrus akakata simu, kwa ujanja akampigia Eddy, simu ilipo pokelewa akaidumbukiza mfukoni mwake.

“Mumenikamata kwa amri ya nani?”

“Raisi ndio ameagiza ukamatwe”

“Kuna sababu ya mimi kunikamata”

“Adrus sisi tunafwata amri, ukituuliza hivyo tutashindwa kukijibu kabisa”

“Sawa”

***

Eddy akakitoa simu yake mfukoni na kukuta ni namba ya Adrus ndio anaye piga kwa haraka akaipokea, cha kushangaza akaanz kusika mazungumzao mbayo yakaanza kumpa wasiwasi, kitendo cha kusikia Adrus amekamatwa kutokana na amri ya Rahab akashangaa sana. Kwa haraka Eddya kakata simu yake na kumpigia raisi Rahab, simu yake ikaita kwa muda kisha ikapokelewa.

“Baby?”

“Mbona umetuma watu wamkamate Adrus kuna kitu gani kinacho endelea?”

“Eddy tafadhali punguza jazba, uliza kwa utaratibu mpenzi wangu?”

“Kwa utaratibu gani Rahab, niambie ni kwa nini umamkamata?”

“Upo wapi?”

“Rahab hilo sio jibu la swali langu”

“Natambua hilo Eddy nijibu upo wapi, usijisahau kumbuka mimi ndio raisi”

Rahab naye alizungumza kwa ukali na kumfanya Eddy kushusha pumzi na kujitahidi sana kushusha hasira yake.

“Nipo ofisini kwangu”

“Kaa kwenye tv yako tuzungumze live”

“Sawa”

Eddy akakata simu huku akimtaazama Shamsa aliye fura kwa hasira.

“Shamsa?”

“Nini?”

“Ninakuomba unisamehee kwa kile nilicho taka kukifanya kwako, haikuwa dhamira yangu kufanya hivyo”

Shamsa hakujibu kitu chochote zaidi ya kumtazama Eddy, akampandisha na kumshusha. Jibu hilo la macho likamfanya Eddy kunyanyuka kwenye sofa, akazunguka hadi kwenye kiti chake, akaka huku akijiweka vizuri uso wake akiufuta futa kwa mikono yake ili hasira aliyo kuwa nayo isionekane kwa Rahab. Akawasha compture yake aina ya Mac, akakuta picha za video za viongozi wanne, wawili wakiwa ni kutoka Marekani. Raisi Dustan, general wake wa ulinzi na raisi Rahab.

“Habari zenu”

Eddy alizungumza huku akijiweka sawa.

“Salama makamu wa raisi”

General alijibu.

“Eddy hichi ni kikao cha viongozi wa mataifa mawili, Tanzania na Marekani. Kuna mashambulizi makubwa ya kigaidi yametokea nchini Marekani, na hadi sasa hivi tunavyo zungumza ni zaidi ya watu elftu tatu wamefariki dunia. Mashambulizi yote yamepangwa na kikundi cha Al-Quida, moja ya sababu kubwa ni kutokana na kazi walio ifanya vijana wawili ambao ni Naomi na Adrus kule nchini Pakistan. Hayo ni maelezo mafupi ambayo yapo kwenye hichi kikao hapa”

Raisi Rahab alizungumza kwa sauti ya upole haku akimtazama makamu wa raisi Eddy.

“Habari bwana Eddy”

“Salama muheshimiwa raisi”

“Tumezungumza mengi na raisi wako hapa, moja ikiwa ni kuhakikisha kwamba Adrus anawekwa chini ya ulinzi maalumu ambao hauto weza kuliletewa taifa lako matatizo na hichi kikundi. Pia Adrus atakuwa ni master plan mzuri ambaye anaweza kutusaidia kuhakikisha kwamba tunakipata hichi kikundi cha Al-Quida na kukifuta kabisa”

Eddy akajikuta akiyang’ata meno yake kwa hasira kwani hichi anacho kisikia hapa kinakwenda kuvuruga kila kitu katika mpango wa kumuokoa mwanaye na Sa Yoo.

“Tulihitai kuivamia Pakistani kwa sasa ila tumeshauriana tuweze kumchuku Adrus ili aweze kutupa baadhi ya mbinu ili kuepusha vita ambayo itakwenda kua maelfu ya watu pasipo sababu za msingi”

“Eddy nimesha idhinisha kumtoa Adrus ili tuweze kupambana na janga la ugaidi duniani”

Eddy akakosa hata cha kuzungumza zaidi ya kutingisha kichwa kukubaliana na kile alicho kizungumza raisi wake.

“Tunashukuru sana na tutaendelea kuwapa taarifa kwa kila jambo litakalo kuwa linaendelea”

“Sawa”

Eddy akazima computer yake na kuachia msonyo mkali hadi Shamsa aliye jawa na msongamamo wa mawazo akastuka.

“Nini?”

Shamsa aliuliza huku akikaa kitako vizuri. Eddy hakuzungumza kitu chochota, kwa hasira akasukuma kila kitu kulichopo juu ya meza yake na kuanguka chini.

“Agrahaaaa”

Eddy alilia kwa uchungu sana huku hasira ikizidi kumpanda, Shamsa kwa haraka akanyanyuka kwenye sofa na kumsogelea Eddy huku mapigo ya moyo yakimuenda mbio sana.

“Eddy una nini?”

Shamsa alizungumza kwa hasira baada ya kunaza kuona matone ya damu yakitoka puani mwa Eddy. Shamsa kwa haraka akakiweka kitambaa chake puani mwa Eddy.

“Inama, inama”

Shamsa alizungumza huku akimuinamisha Eddy, hasira aliyo nayo Eddy ikazidi kumuendesha kiasi cha kumfanya kichwa cheke kumuua na kupelekea damu kumwagika, kila anavyo waza ni nini atafanya ili kumuokoa mwanaye bado hajapata jibu.

“Eddy niambie ni nini kinacho endelea”

Shamsa alizungumza huku machozi yakimwagika, hasira ya kuchukia kwa nini mwanaye atekwe ikayayuka moyoni mwake, jukumu la kumsaidia mwanaume anaye mpenda kwenye maisha yake likautawala moyoni mwake.

“Waseng** hawa, nawachukia”

“Kina nani jamaniii Eddy si uniambieeee”

Eddy akanyanyuka huku akiwa amekishika kitambaa alicho wekewa puani, akaingia kweye choo kilichopo humu ndani ya ofisi yake huku Shamsa akimfwata kwa nyuma.

“Inama angalia damu isije ikakuchafua shati”

Shamsa alizungumza huku akimshika Eddy mgongoni. Eddy akainamia sinki la kunawia mikono lililopo humu chooni.

“Ngoja nimpigie daktari aje?”

“Acha”

“Baby huwezi kuwa hivyo”

“Acha nimekuambia, usimwambie hata Phidaya”

Eddy alizungumza kwa sauti nzito huku akimkazia macho Shamsa, aliye baki ameshikwa na bumbuazi. Eddy akendelea kuinama hadi damu ikakata, akanawa uso wake huku akiisafisha pua yake. Alipo hakiksha yupo vizuri wakatoka humu chooni.

“Pole”

Shamsa alizungumza huku akimtazama Eddy anaye onyesha dhairi kwamba ana hasira bado.

“Asante, rudi nyumbani sasa hivi, ninakwenda ikulu sawa”

“Na hili swala la mtoto Eddy inakuwaje?”

“Nitajua jinsi ya kulishuhulikia sawa?”

Shamsa akajibu kwa kutingisha kichwa, anakubali kwa singo upande kutokana hana jinsi ya kufanya kwani mwenye familia ndio amezungumza.

“Hakikisha kwamba Phidaya hafahamu chochote, unatambua matatizo yake, ikiwezekana pia jariu kucheza na simu yake, meseji na simu zinazo ingia hakikisha kwamba unajua ni nani anaye piga, tukicheza vibaya, kila jambo linaharibika umenielewa?”

“Nimekuelewa”

Eddy akamtazama Shamsa kuanzia juu hadi chini, akamshika kiuno na kumsogeza karibu yake. Wakatazamana kwa muda kidogo, Eddy akazipeleka lipsi zake kwenye midomo ya Shamsa na kuanza kumnyonya, taratibu Shamsa akakubaliana na kitendo hicho kwa maana ni mzazi mwenzake na tangu siku aliyo mvunja bikra hakuweza kulipata penzi lake. Shamsa hisia za kimapenzi zikamshika kabisa na kujikuta akianza kufuangau mkanda wa suruali ya Eddy.

“Hei Shamsa kuna ishu nahitaji kwenda kuishuhulikia sasa hivi, tutafanya siku nyingine”

“Oooohooo kidogo nipe baby”

Shamsa alizungumza kwa sauti ya mahaba huku akikazana kuhakikisha kwamba anaufungua mkanda wa Eddy, Shamsa kwa papara zake akafanikiwa kuingiza mkono wake ndani ya suruali ya Eddy akamshika jogoo aliye simama kikamilifu.

“Ohooo, aaiiissssiiiii…..”

Shamsa alitoa miguno ya kichokozi huku macho yakimlegea sana, Eddy kwa haraka akamlaza Shamsa juu ya sofa kubwa la hapa ofisini kwake. Shamsa kwa haraka akavua suruali yake na kubakiwa na bikini, Eddy akaisogeza pembeni bikini hiyo, hakuwa na haya ya kumuandaa Shamsa kwani tayari kitumbua kimesha lowa kwa maji. Eddy akaanza kukishuhulikia kitumbua cha Shamsa huku akihakikisha kwamba anakitafuna kisasa sawa. Shamsa akazidi kutoa miguno ya kimahaba huku akihema juu juu kama mtu aliye kimbia mbio za marazoni.

“Nakupenda baba Junion”

“Nakupenda pia”

Eddy akamgeuza Shamsa na kumuinamisha, akakishika kiuno cheke na kuandelea kukila kitumbua, ubaya ni kwamba asubuhi na mapema amatoka kumshuhulikia raisi Rahab, ambaye naye nyeg** zilimpanda.

“Akgra…..argrgraa”

Shamsa alilia huku akikiwa ameking’ata kimto kidogo cha sofa na kusababisha sauti yote kuishilia ndani ya kijimto hicho.

“A…h…na….mwa…..g……”

Eddy alilamika huku akijisikia raha ambayo wanaume wote huipata wakifika katika muda kama huo.

“Mwaga”

Spid ya Eddy ikaanza kupungua baada ya waarabu weupe kuzama ndani ya kitumbua cha Shamsa, taratibu Eddy akajikuta akilala mgongoni mwa Shamsa huku shati zima alilo livaa likijaa jasho jingi sana.

“Asante mpenzi wangu, nimekosa hii raha kwa muda mrefu sana”

“Asante na wewe”

“Nimeridhika kidogo, usiku nahitaji tena”

Eddy akabaki amemtolea macho Shamsa, kwani kwa mikiki mikiko yote aliyo mpa ila anadai kwamba hajaridhika.

“Sawa, nenda nyumbani ukafanye kama nillivyo kuambia”

“Sawa baby”

Eddy taratibu akamchomoa jogoo wake anaye anza kulala taratibu kutokana na kumaliza kufanya kazi yake. Shamsa akajilaza kifudi fudi huku akimtazama Eddy anaye buruza suruali yeka chini kwa mguu mmoja ambao bado haujatoka kwenye suruali yake.

“Ivue hiyo suruali bwana usiingie nayo huko chooni hiyo”

Shamsa lizungumza na kumfanya Eddy kuuchomoa mguu huo na kuingia fafuni akiwa na shati pamoja na viatu vyake tu. Akasimama kwenye kioo na kujitazama.

“Mmmm kazi ninayo”

Eddy alizungumza huku akianza kunawa mikono yake, akashukua toilet pepar na kumfuta jogoo wake, akamnawisha vizuri kisha akamalizia kumkausha kausha na karatasi hizo za chooni. Shamsa akaingia chooni humo na kijiarufu cha Eddy kikamfanya agune.

“Una guna nini?”

“Unanuka jasho la mapenzi hivi hivi”

Eddy akajaribu kujinusa maeneo ya kwapani na kuivuta harufu hiyo.

“Tuoge ndio tutoke, huwezi kwenda ikulu ukiwa hivyo na mijijasho yako, kila mtu atajua kwamba tumetoka kutomb**a”

“Jamani”

“Jamani nini tuoge, hembu tazama mashagaw** yako yanavyo nichuruzika huku kwenye mapaja”

Eddy hakuzungumza chochote zaidi ya kuangalia maumbile mazuri ya Shamsa ambaye kipindi anakutana naye alikuwa bado ni mtoto mdogo sana.

‘Kweli wanawake sio wezetu, juzi tu kifua kilikuwa hakijaja’

“Unaniangalia nini tuoge”

“Nivue shati”

Taratibu Shamsa akamvua Eddy shati lake, akamvua na viatu pamoja na soksi akavitoa chooni humo, taratibu wakanaza kuogeshana, upendo ambao kwa mara ya kwanza Eddy hakuujali ukaanza kumingia moyoni mwake. Uzuri wa Shamsa unamfanya ajiapize moyoni mwake kuto kumuacha na kujisifia kwa dodo zuri alilo lipata. Wakamaliza kuoga na kutoka bafuni homo.

“Sasa utavaje hilo shati lililo jaa majasho hivyo?”

“Nitapata wapi jengine la kubadilisha”

“Mmmm”

“Ndio hivyo, na hili jambo ufanye siri, ujinga wa kwenda kumuambia Phidaya sitaki tabu sawa”

“Sasa Eddy unahisi kwamba nitakwenda kumuambia Shamsa kwnai mimi ni mtoto mdogo”

“Haya mwaya”

Wakamaliza kuvaa nguo zao, walipo hakikisha kwamba wapo vizuri, wakatoka ofisini humo.

“Hei hakikisha ofisi yangu inapangwa vizuri”

Eddy alimuambia sekretari wake huku wakiingia ndani ya lifti na Shama. Wakashuka hadi gorofa ya chini, Eddy akamkabidhi Shamsa kwa mlinzi wake mmoja na ili ampeleke nyumbani, kisha yeye akingia kwenye msafara wa gari zake nne na kuondoka katika eneo hili.

“Hei nahitaji shati, piteni kwenye duka lolote la kiume munichukulie shati jeupe”

“Sawa mkuu”

Kila mtu akashangaa msafara wa makamu wa raisi kusimama katika maduka ya hapa Posta, akashuka mlinzi mmoja, akaingia kwenye moja ya duka la nguo za kiume, akanunu shati linalo endana na mwili wa Eddy kisha akarudi kwenye gari, na kumkabidhi Eddy hyku wakiondoka katika eneo hili. Eddy akaanza kubadilisha shati hilo alipo hakikisha amelivaa vizuri, akavaa moja ya koti lake analo liacha ndani ya gari lake hili. Msafara wake ukafika ikulu. Eddy hakusubiriwa hata kufunguliwa mlango, akashuka kwenye gari.

“Agent Adus amesha fikishwa hapa?”

Eddy alimuuliza mmoja wa walinzi.

“Ndio muheshimiwa”

“Nipeleke alipo”

Eddy akaongozana na mlinzi huyo hadi kwenye ofisi alipo pelekwa Adrus na kumkuta akiwa amekaa kwenye kiti.

“Muheshimiwa?”

Adrus alizungumza huku akisimama.

“Kaa, wamekuambia sababu ya kuletwa hapa?”

“Wameniambia ni raisi ndio ameagiza”

“Tusileteane upuuzi”

Eddy alizungmza huku akitoka ofisini humu, moja kwa moja akaelekea ilipo ofisi ya Rahab, bila hata ya kubisha hodi akaingia ndani, akamkuta Rahab akizungumza na balozi wa Marekani hapa nchini Tanzania.

“Eddy heshima ifwate mkondo wake?”

“Balozi tupishe”

Eddy alizungumza kwa hasira na kumfanya balozi huyu kumtazama raisi kwani raisi Rahab ndio aliye muita ndani ya hiyo ofisi.

“Eddy ninakuomba usubiri nje?”

“Hei mama nimekuambia tupishe, ondoka ninahitaji kuzungumza na raisi wangu”

“Kaa huyu ni mgeni wangu sawa, kuwa na heshima Eddy”

Rahab alizungumza kwa hasira huku akisimama kwenye kiti chake. Eddy akatabasamu kidogo huku akimtazama balozi huyu, kisha akamtazama Rahab.

“Nimekuelewa muheshimiwa raisi. Ila kuanzia hivi sasa ninajivua madaka ya kuwa makamu wa raisi wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania. Asante”

Eddy baada ya kumaliza kuzungumza maneno hayo akaanza kuelekea mlangoni kwa hatua za haraka na kumfanya Rahab kuanza kutetemeka mwili mzima kwani hakujua hasira yake ingemfanya Eddy kuchukua maamuzi ambayo hakuwahi kuyatarajia kuyasikua kutoka kinywani mwa Eddy siku hata moja.



Eddy akaufungua mlngo na kuubamiza kwa nguvu hata walinzi walio simama mlangoni kmwa ofisi ya Rahab wakabaki wakishangaa kwani hawakutegemea kukiona kitendo kama hicho kwa makamu wa raisi. Rahab akajikuta nguvu zikimuishia na kukaa kwenye kiti chake. Eddy moja kwa moja akatoka nje huku walinzi wake wakimfwata.

“Hei hamuna haja ya kunilinda tena”

Eddy alizungumza huku akiwageukia walinzi wake walipo nyuma yake. Walinzi wakabaki wakiwa wameduwaa huku kila mmoja akiwa na kigugumizi asielewe ni kitu gani kinacho endelea. Eddy akaelekea kwenye moja ya gari linalo tumika katika msafara wake.

“Nipe funguo”

Eddy alizungumza kwa msisitizo na kumfanya dereva kushangaa.

“Nimekuambia nipe funguo na utoke ndani ya gari”

Eddy alizidi kufoka na kumfaya dereva kumkabidhi funguo na kushuka kwenye gari.

“Na nyinyo nimewaambia kwamba sihitaji munilinde tena kuanzi hivi sasa mimi sio makamu wa raisi wa nchi hii nimejiudhuru sawa?”

Hapakuwa na mlinzi aliye jibu swali lolote zaidi ya wote kukaa kimya wakiduwaa. Eddy kwa haraka akafungua mlango wa upande wa dereva, akaingia na kuufunga kwa nguvu, akawasha gari, kwa haraka akalirudisha nyuma, akaliweka sawa, na kundoka kwa kasi huku akilililenga geti la kutoka hapa ikulu, kwa haraka walinzi wakaufungua geti na Eddy akaondoka kwa kasi sana huku kifua kikimpanda na kushuka akifikiria jinsi ya kumsaidia mwanye ambaye yopo mikononi mwa John adui yake mkubwa sana, kitu kingine kinacho muumiza akili ni juu ya John kuwa na viongo vyake kamili ikiwa alimkata miguu pamoja na mikono yake kipindi alipokuwa na Sheila.

***

Dokta Ranjiti na walinzi wake wawili wakafika nchini Kenya kwa ndege binafsi, hawakutaka kupoteza muda, walicho kifanya ni kukodisha gari maalumu lililo wapeleka hadi mpakani mwa Tanzania na Kenya kupitia mkoani Arusha. Wakakaguliwa hati zao za kusafiri pamoja na visa zao zinazo onyesha kwamba wanaingia nchini Tanzania kwa ajili ya kutembela mlima wa Kilimanjaro. Hapakuwa na shaka aina yoyote kwao na wakaruhusiwa kuingia nchini Tanzania.

‘Eddy jiandae nilazima nimrudishe Phidaya wangu mikononi mwangu’

Dokta Ranjiti alizungumza huku akitazama jinsi miti inavyo kwenda kasi kutokana na gari alilo panda kuendeshwa kwa mwendo wa kasi sana. Hawakuchukua muda mrefu wakafika jijini Arusha, wakafika katika hoteli ambayo tayari dokta Ranjiti alisha weka oda ya vyumba viwili, chake na cha walinzi wake.

“Pumzikeni sasa hivi ila hakikisheni kwamba munaitafuta namba ya Phidaya hadi munaipata, nina lala hadi jioni hakikisheni kwamba muipa”

“Sawa mkuu”

Dokta Ranjiti akaingia chumbani kwake na walinzi wake wakingia katika chumba cha pili kwa ajili ya kujipumzisha kwani ni usiku mzima tangu walipo toka nchini Uingereza hawakuweza kulala ndani ya ndege.

***

“Ulikuwa wapi?”

Phidaya alimuuliza Shamsa mara baada ya Shamsa kufungua mlango na kuingia ndani.

“Nilitoka na baba”

Shamsa alizungumza kwa unyonge sana huku akikaa kweye moja ya sofa lililopo hapa sebleni.

“Mbona kama unaumwa?”

“Hapana nipo vizuri tu mama”

Shamsa alizungumza huku akijikaza kutokuonyesha hisia za unyonge wake. Phida ayaksogela Phidaya na kumgusa shingoni mwake kwa kutumia kiganja chake.

“Joto limekupanda, ngoja nimpigie daktari”

“Hapana mama, nipo vizuri. Camila yupo wapi?”

“Amelala, umekunywa chai?”

“Hapana”

“Jamani ila kwa nini unakuwa hivyo, twende ukanywe chai basi”

“Mama sijisikii kula”

“Kwa nini hujisikii kula?”

“Nitakula baadae”

Shamsa alizungumza huku akinyanyuka kwenye sofa alilo kalia, akaelekea ndani kwake na kujitupa kitandani, Phidaya akaingia huku akionekana kujawa na maswali mengi kichwani mwake kwani anamfahamu vizuri Shamsa na hajawahi kumuona akiwa katika hali kama hiyo.

“Shamsa”

“Beee”

“Kuna kitu gani kinacho endelea”

Phidaya alizungumza kwa sauti ya chini huku akimtazama Shama aliye ilaza kifudi fudi.

“Kivipi mama?”

“Kwa maana sio kawaida yako kutoka asubuhi pasipo kuaga”

Kabla Shamsa hajazungumza kitu chochote simu ya Phidaya ikaanza kuita, kwa haraka Shamsa akakurupuka kitandani na kushuka, kitendo kilicho mshangaza Phidaya.

“Ninakwenda kukuchukulia simu”

Shamsa alizungumza huku akitoka ndani humu, moja kwa moja akakimbilia sebleni, akaichukua simu ya Phidaya inayo ita juu ya meza. Shamsa akashusha pumzi nyingi mara baada ya kuina namba ya Eddy ndio inayo piga, akarudi chumbani kwake na kumkabidhi Phidaya simu.

“Ni baba”

Shamsa alizungumza huku akijitupa kitandani, kwa haraka Phidaya akaipokea simu ya mume wake.

“Honey”

“Upo nyumbani?”

“Ndio”

“Pakini nguo zenu kwenye mabegi tunaondoka nyumbani hapo”

“Haaaa……!!!”

Mshangao wa Phidaya ukafanya Shamsa kushangaa na kukaa kitako kitandani.

“Nimekuambia kusanyeni kila kitu tulicho ingia nacho hapo jana na tunahama hapo”

“Ila Eddy mbona umestukiza kiasi hicho, tunaondoka tunakwenda wapi sasa”

“Phidaya sihitaji maswali mengi ikiwa nilicho kizungumza ni Kiswahili cha kueleweka sawa”

Eddy alizungumza kwa kufoka kiasi cha kuifanya sura ya Phidaya kubadilika na kukosa furaha kabisa. Simu ikakatwa na kumfanya Phidaya kushusha pumzi nyingi sana.

“Kuna nini?”

Shamsa aliuliza huku akikaa kitako kitandani.

“Baba yako anasema tukusanye kila kilicho chetu na tunaondoka leo”

“Tunaondoka…..!!!?”

“Yaa hata mimi mwenye nina shangaa”

“Heeee amechanganyikiwa au?”

“Mmmmm sijui mie, nimesha jichokea na haya maisha ya kuhama hama jamani”

“Mmmm ngoja tumsubirie aje”

“Twende kwanza ukanywe chai”s

Shamsa hakuwa na haja ya kumkatalia tena Phidaya akashuka chumbani na kutoka chumbani humo.

***

Mawazo ambayo raisi Dustan na mkuu wa jeshi walikuwa wakiyawaza yameweza kufanya kazi kwani yule walite kuwa wakimuhitaji wamempata na sasa wanasubiria ubalozi wao wa nchini Tanzania kuweza kumsafirisha Adrus kuja nchini Marekani.

“Kwa kupiti hiyo kijana nina uhakikia kwamba kila jambo litakwenda kuwa sawa”

Mkuu wa jeshi alizungumza huku akimtazama raisi Dustan.

“Ila tunakwenda nje ya muda kwa maana mwanagu wamemshikilia bado na sijui ni kitu gani watakwenda kukifanya katika muda unao fwata”

“Nina imani kila jambo litakwenda sawa, na gaidi tuliye mkamata nina imani kwamba atakuwa ni msaada mkubwa sana kwatu”

“Hakikisheni kwamba muna muhoji, na akishindwa kuwaeleza kitu cha kueleweka mpigeni risasi afe”

“Sawa muheshimiwa raisi”

Mkuuw a jeshi akatoka ofisini mwa raisi Dustan moja kwa moja akaelekea katika ukumbi mkubwa wa mikutano kuhakikisha anayashuhudia majiano yanayo hojiwa na vijana wake yanayo onekana kwa njia ya Tv kubwa iliyomo katika ukumbi huu.

***

Kitendo cha wanajeshi wengi wa kundi la IS(Islamic State) walio ungana na kikundi cha Al-Quida kushindwa kutimiza adhima ya kumkamata Naomi, kikawapandisha hasira kali sana.

“Kaka inabidi kumchinja huyu binti wa raisi”

Omary alimuambia kaka yeke, Hamad Tariq mkuu wa kikundi cha Al-Quida.

“Hapana muda wake wa kufa bado, ninajua Marekani wana mpango mwengine dhidi yetu ila ninahitaji kuwaonyesha kwamba na sisi tunaweza”

Hamad Tariq alizungumza kwa hasira huku akimtazana mdogo weke, malango wa ofisi yake iliyopo chini ya Ardhi katika nchi ya Pakistani ukafunguliwa, akaingia mtaalamu waneye mtegemea katika mswala ya teknolijia ya mawasiliano.

“Mkuu kuna video hapa nahitaji kuwaonyesha”

Dulah alizungumza huku akiwa ameshika tablate kubwa, akaimkabidhi Hamad Tariq, wakanza kuyatazama mazungumzo ya raisi Dustan akiwa na mkuu wake wa majeshi pamoja na raisi Rahaba wa nchini Tanzania.

“Mazungumzo haya yamefanyika lini?”

“Yamefanyika leo dakika thelathini zilizo pita, nimayaiba katika mtandao wa ikulu”

“Ni kijana gani wanaye mzungumzia hapa?”

Dulah, akaisimamisha video hiyo na kuiweka picha ya Adrus, wote walipo inaoa wakastuka sana kwani kijana huyu ni alisaidiana kabisa na Naomi katika kumuua mmoja wa viongozi wake.

“Anaitwa Adrus Maldin ni komandoo mwenye umri mdogo na mafunzo ya hali ya juu. Chanzo kikubwa cha kifo cha mjomba wako ni huyu, sasa Wamarekani wamakubaliana na Tanzania kumchukua kijana huyo. Liati wakimpata nina imani kwamba tupa hatarini”

Bwana Hamad Tariq akashusha pumzi nyingi huku akiitazama picha ya Adrus akiwa amevalia mavazi ya kijeshi.

“Kwa sasa yupo wapi?”

“Bado yupo nchini Tanzania, ila sijajua yupo katika kitengo gani, ila makubaliano tukiyaacha yakamilike basi sisi tupo hatarini. Kitu kingine ni kwamba huyu Adrus ana mahusiano ya kimapenzi na Naomi so atafanya kazi kwa juhudi kubwa kuhakikisha kwamba analipiza kisasi cha sisi kumshambulia mpenzi wake”

“Nchini Tanzania hivi tuna mtu ambaye anaweza kuifanya hiyo kazi?”

“Labda uwasiliane na madam LIVINA ili aweze kutupa msada katika kwa kutumia wasichana wake tunaweza kufanikisha tukio hilo kama ilivyo kuwa katika tukio la kumteka Charity”

Hamad Tariq akaka kimya kidogo huku akifikiria ushauri alio pewa na Dulah.

“Ila Livna atahitaji pesa nyungi sana kama alivyo hitaji katika tukio la kumteka Charity?”

“Kaka pesa sio muhimu sana, kumbuka huyo tunaye mshuhulikia ni mtu hatari, hembu piga picha Wamarekani wakimtumia, ila kuto kupoteza wanajeshi zaidi tumtumie Livna na jeshi lake”

“Sawa nimewaelewa hemu fanya mawasiliano na Livna”

***

“Livna”

“Mmmmmmmm”

“Mjukuu wangu hali yangu sio nzuri…..ninakwenda kufa mjukuu wangu”

Bibi Ying muanzilishi wa kundi kubwa la wasichana wanao fanya kazi za kijasusi alizungumza huku akiwa amemshika Livna msichana anaye mpenda na amemkabidhi majukumu yote ya kuongoza kundi kubwa la wezake ambalo makazi yao ni ndani ya meli kubwa sana iliyopo katikati ya bahari ya Hindi.

“Bibi usiseme hivyo una niogopesa”

Livna alizungumza huku machozi yakimlenga lenga usoni mwake.

“Siwezi kupona saraatani hii ya damu, hata nikifa leo hakikisha kwamba unawaongoza wezako vizuri, hakikisha kwamba unazidi kulete wasichana wapya hawa watoto kuhakikisha kwamba kundi linazidi kukua”

“Sawa bibi nitafanya hivy….”

Livna hakuimalizia sentensi yake, akaitoa simu yake mfukoni baada ya kuingia ujumbe mfupi. Kwa haraka akaitoa mfukoni simu yake huku akiwa na wasiwasi mwengi kwani ana amini kazi walio ifanya vijana wake katika kumteka Charity ni lazima kwa sasa itakuwa imechukua vichwa vingi vya habari duniani mwote na vijana wake watakuwa wanatafutwa. Livna akashusha pumzi nyingi na kasi ya mapigo ya moyo iliyo sababishishwa wasiwasi, yakapungua, kwani meseji hiyo inatoka kwa kijana wake wa ndani ya hili meli akimuhitaji akimueleza kwamba kuna simu yake muhimu.

“Bibi ninakuja”

“Sawa”

“Dokta muangalie bibi sawa”

“Sawa”

Livna akanyanyuka kwenye kiti alicho kalia na kutoka chumbani humu, kwa haraka akelekea gofani katika meli hii, sehemu yenye chumba cha wamasiliano, kwa haraka akiangia katika chumba hicho.

“Kuna nini kinacho endelea?”

Livna alizungumza huku akimtazama msichana anaye shuhulika na swala hilo.

“Kuna simu kutoka kwa Hamad Tariq”

“Anahitaji nini ikiwa mimi na yeye tumesha maliza kazi?”

“Sijajua”

Livna akaichukua maalumu ambayo simu zote zinazo ingia kitika simu hiyo ya kazi haziwezi kunaswa na mitambo ya satelaiti.

“Ndio”

Livna alizungumza kwa msisitizo huku akiwa ameiweka simu yake sikioni mwake.

“Ninahitaji msaada wako?”

“Msaada wangu upi?”

“Kuna picha zitaingia hapo kwenye email yenu, huyo kijana ninamuhitaji kabla wamarekani kumpata”

Picha ya Adrus ikaonekana kwenye tv kubwa iliyomo ndani ya chumba hichi.

“Ni nani?”

“Nimiongoni mwa kijana aliye muua mjomba wangu katika mashambulizi nchini Pakistani, sasa ninamuhitaji”

“Tariq vvijana ninao, ila hata siku mbili hazijapita tangu waweze kuifanya kazi yako, sasa unavyo zungumza hivyo unanipa waswasi, ni kwa nini usiwatumie vijana wako?”

“Livna kumbuka kwamba vijana wangu wote ni waarabu na hadi sasa hivi nina imai kwamba tutakuwa tunatafutwa kila sehemu, nikiwatumia wao sinto fanikwa kama ilvyo kuwa katika katika shambulizi la hospitalini”

Livna akaka kimya huku akifikiria ombi la Hamad Tariq.

“Mimi na Tanzania hatuna ubaya wowote, na Tanzania nipo karibu nayo, sasa sihitaji kuingia nayo katika matatizo”

“Huwezi kuingia nayo kwenye matatizo kwa maana ni mtu mmoja ndio tunamuhitaji, na sisi ndio tutajitokeza na kusema kwamba tumehusika na kumteka kijana wao”

“Una kiasi gani cha pesa?”

“Nina dola milioni moja”

“Siwezi kuichukua hiyo tenda. Wafanye vijana wako la sivyo pandisha dau”

“Basi zungumza wewe unahitaji kiasi gani?”

“Dola milioni tano, huna basi mimi na wewe hauwezi kufanya kazi”

“Basi nipo tayari kukupatia?”

“Naamini unaifahamu akaunti yangu, ingiza hizo pesa, kisha utanitumia detail za wapi alipo huyo kijana na mimi nitajua nini cha kufanya sawa”

“Sawa”

Livna akakata simu huku akiwa amejawa na tabasamu pana usoni mwake kwani chanzo cha kujipatia pesa ili kuongoza kundi hilo lenye wasichana zaidi ya elfu thelathini ni kufanya matukio makubwa kama hayo ambayo na kujipatia pesa nyingi sana.

***

Eddy akasimamisha gari nje ya nyumba anayo ishi kwa haraka akashuka na kuanza kuelekea ndani kwa mwendo wa kasi sana. Akafunguliwa mlango na walinzi walio simama hapo, macho yakamtoka baada ya kuwakuta Phidaya na Shamsa wakiwa wamekaa katika meza ya chakula wakinywa chai taratibu.

“Mumesha jiandaa?”

Eddy alizungumza kwa ukali huku akiwa amefura kwa hasira, ugonjwa wa hasira ambao kwa kipindi kirefu alijitahidi kuukabili, taratibu umeenza kumnyemelea.

“Eddy una nini mume wangu?”

Phidaya alizungumza huku akisimama kwneye kiti alicho kikalia.

“Nahitaji nikamuokoe mwanangu”

Maneno ya Eddy yakaustua moyo wa Shamsa, aliye jikuta akikiweka kikombe cha chai mezani hata kabla hajapiga funda la chai alilo kuwa amelidhamiria kulinywa.

“Mwanao……Mwanao yupi….!!!!?”

Shamsa alizungumza huku akiwa ameshangaa sana, kwani mtoto wake yupo chumbani amelala. Macho ya Eddy yakaanza kujawa na ukungu mwigi ulio msababisha kuanza kuyumba huku akiyafumba fumba macho yake, damu zikaanza kumtoka puania kitendo kilicho mstua Phidaya pamoja na Shamsa, galfa Eddy akaanguka chini na kumfanya Phidaya kukimbilia eneo alilo anguka Eddy huku akipiga kelele kubwa ya kuomba msaada kwa walinzi waliopo nje ya nyumba yao hii.


Kwa haraka walinzi wakaingia ndani, kwa haraka wakaanza kumpa huduma ya kwanza Eddy huku wakimfungua mkanda wa suruali pamoja na vifungo vya shati lake. Wakambeba Eddy hadi katika gari lake alilo kuja nalo.

“Shamsa kamchukue Camilia”

Phidaya alizungumza huku akikimbilia nje alipo pelekwa mume wake, akaingia katika gari alilo ingizwa Eddy, gari moja ya walinzi yenye king’ora ikatangulia mbele, na kuandoka kwa kasi katika jumba hili huku ikiwasha king’ora kusafisha njia. Shamsa akaingia chumbani, hakijali Camila amelala, akamnyanyua hivyo hivyo na kumbeba, kwa haraka akatoka nje na yeye akaingia kwenye gari jengine na wakaanza kufukuzia gari mbili zilizo tangulia. Wakafanikiwa kufika katika hospitali ya Muhimbili, moja kwa moja Eddy akapakizwa katika kitanda cha wagonjwa na kukimbizwa katika chumba cha matibabu. Phidaya kwa haraka akaichukua simu yake na kumpigia raisi Rahab.

“Wifi”

Phidaya aliita huku sauti ikimtetemeka sana, jambo lililo mstua Rahab ambaye muda wote alikuwa akijitahidi kumpigia simu Eddy ila Eddy alikata na mwisho akazima simu.

“Niambie wifi yangu?”

“Mume wangu ameanguka gafla na tupo hapa Muhhimbili”

“What….!!?”

“Ndio”

“Ok, ok ninakuja sasa hivi”

Simu ikakatawa na kumfanya Phidaya kuanza kuiminya kwa kiganja cha mkono wake wa kulia kama mtu anaye kamua kipande cha chungwa. Uchungu mwingi umetawala moyoni mwake, kwani katika maisha yake yote na mume wake hawajawahi kuishi kwa furaha zaidi ya matatizo yanayo wakabili kila siku. Machozi yakaanza kumtiririka mashavuni mwake huku akijitahidi kumuomba Mungu aepushe tatizo hili lililopo mbele ya mume wake kipenzi, mwanaume aliye dumu naye kwa muda mrefu katika shida na raha.

***

“Niandalieni msafara ninakwenda Muhimbili sasa hivi”

Raisi Rahab alizungumza kwa haraka huku akimuambia mlinzi wake wa kike.

“Andaeni msafara madam raisi anatoka. Poiti ya mwisho ni Muhimbili”

Mlinzi huyo alizungumza kupitia kinasa sauti chake alicho jifunga katika mkono wake wa kulia. Wakatoka nje na kukuta gari sita aina ya Range Rover Sport zikiwa zimepangwa katika mstari mmoja, walinzi tauari walisha jiandaa huku pikipiki mbili kubwa za askari usalama barabarani zikiwa tayari zimesha tagulia kwa ajili ya safari hii ya dharura. Mlinzi wa raisi Rahab akamfungulia mlango na Rahab akingia, walinzi wote wakaingia kwenye gari zao na safari ya kuelekea hospitali ya Muhimbili ikaanza. Raisi Rahab akatoa simu yake mfukoni, akaitafuta namba ya simu ya daktari mkuu wa hospitali ya muhimbili na kumpigia.

“Muheshimiwa raisi”

“Dokta Benjamini, makamu wa raisi ameletwa hapo hospitalini una taarifa hiyo?”

“Ndio muheshimiwa tunaendelea kumuhudumia”

“Hali yake inaendeleaje?”

“Kwa sasa ni ngumu kuzungumza muheshimiwa, ila baada ya muda tunaweza kufahamu tatizo halisi la muheshimiwa”

“Hakikisha kwamba hali yake inakuwa salama sawa”

“Sawa mkuu”

Rahaba akata saimu ba kushusha pumzi nyingi sana huku akionekana kujawa na wasiwasi mwingi sana, moyoni mwake anajilaumu ni kwa nini ameamua kufanya maamuzi ya peke yake, ikiwa Eddy ni msaidizi wake katika mambo mengi, ukiachilia usaidizi wa kazi ila hata usaidizi wa hisia za mapenzi ni msaada mkubwa sana kwake kwani ni asubuhi ya leo wametoka kuburudishana. Kwa mara ya kwanza mlinzi wa raisi aliye kaa siti ya mbele pembeni ya dereva, akishuhudia raisi akimwaga chozi lake. Ukimya ukatawala ndani ya gari hadi walipo fika katika hospitali ya muhimbili, wakashuka walinzi wote kuimarisha ulinzi kisha mlinzi wa Rahab akawa wa mwisho kushuka, akatazama eneo hili jinsi walinzi wengine walivyo imarisha ulinzi kisha akamfungulia mlango raisi Rahab aliye shuka kwa haraka. Wakaongozana hadi katika chumba anacho fanyiwa matibabu makamu wa raisi, akawakuta Phidaya, Shamsa, Camila pamoja na walinzi wengine wakiwa nje ya chumba hicho. Kwa haraka raisi Rahab akamkumbatia Phidaya ambaye baada ya kumuona Rahab akajikuta akimwagikwa na machozi.

“Wifi mume wangu atakufa?”

“Shiiiiii…..hawezi kufa madaktari watajitahidi kuhakikisha kwamba hali yake inakuwa salama”

Rahab alizungumza huku akimpiga piga Phidaya mgongoni mwake. Wakaachiana taratibu, Rahab akampa mkono Shamsa aliye utazama kwa muda kisha akaupokea jambo lililo mfanya Rahab kuanza kuhisi kuna kitu kinaendela kwa Shamsa.

“Wifi ilikuwaje kuwaje?”

“Alinipigia….alinipigia simu akaniambia ni….ni tukusanye kila kitu…..”

Phidaya akashindwa kumaliza kuzungumza na kuangua kilicho kilicho mfanya Rahab kumkumbatia.

“Basi, basi wifi usilie atakuwa salama”

Rahab akajikuta akiwa mfariji, sauti ya kilio cha Camila ikawafanya Phidaya Na Rahab kuachiana na kutazamana Camila, taratibu Phidaya akachukua mwanaye kutoka mikononi mwa Shamsa kisha akakaanza kumbembeleza.

“Rahab tunaweza kuzungumza?”

Shamsa alizungumza huku akimtazama Rahab usoni mwake. Rahab akamtazama Shamsa kwa muda kisha wakasogea pembeni, sehemu ambayo mazungumzo yao hakuna anaye weza kuyasikia.

“Kuna nini kinacho endelea kwa Eddy?”

“Nikuulize wewe kwa maana wewe ndio unaye muongoza Eddy?”

Rahab akashusha pumzi nyingi huku akifikiria kitu cha kumjibu Shamsa

“Sifahamu, ila kuna maswala ya kazi ambayo hutakiwi kufahamu?”

“Hivi unajua ni nini kinacho endelea eheee?”

Shams alizungumza kwa msisitizo huku akimkazia macho Rahab ambaye akajikuta akiwatazama walinzi walio simama mita chake kutoka walipo.

“Nitajuaje kinacho endelea pasipo kuambia ni nini kinacho endelea”

“Wewe si unauwezo wa kufikiria kila kinacho endelea na hili fikiria katika hisia zako”

Shamsa baada ya kumaliza kuzungumza maneno hayo akaondoka na kumuacha Rahab akiwa amejawa na maswali mengi kichwani mwake.

***

“Habari yako bwana Adrus”

Balozi wa Marekani alizungumza huku akimtazama Adrus aliye kaa huku mikono yake akiwa ameiweka juu ya meza.

“Salama”

“Ndani ya saa moja kuanzi hivi sasa utakwenda nchini Marekani, sababu moja kuu ni kwenda kusaidiana na vitengo vilivyopo hapo kuhakikisha kwamba tunawapata magaidi wa kikundi cha Al-quida na Islamic State, nina imani kwamba wewe unafahamu sana kuhusiana na vikundi hivi”

Adrus akaka kimya pasipo kuzungumza chochote huku akimtazama balozi huyu.

“Hii ni barua kutoa kwa raisi wako”

Adrus akaifungua barua iliyo kunjwa vizuri na kuyasoma maelezo ambayo raisi Rahab amemruhusu kuelekea nchini Marekani na kutoa ushirikiano na serikali hiyo kama alivyo agizwa. Kwa upande mmoja ni habari nzuri kwa maana ni naafasi aliyo kuwa anaitamani sana kwani ana shahuku kubwa ya kumuona mpenzi wake Noami.

“Mumezungumza na makamu wa raisi?”

“Analifahamu hilo na amekubaliana nasi”

“Basi kama ni hivyo nipo tayari kwa hilo, ila kabla sijaondoka ninahitaji kuonana na mama yangu, kama inawezekana akaletwe sasa hivi”

“Unaweza kutupatia picha ili kama ni kuletwa akaletwe uwanja wa ndege?”

“Ndio”

Adrus akamuonyesha balozi wa Marekani picha ya mama yake.

“Kwa sasa yupo wapi?”

“Maeneo ya Kariakoo”

“Basi tutamchukua muda wowote kuanzi hivi sasa”

“Japo nchini yangu imekubaliana na mimi kufanya kazi nanyi ni kitu gani mutakifanya kwa ajili ya mama yangu kwa maana yeye ndio mtu aliye nisaidia mimi kufika hapa nilipo”

“Unahitaji tumfanyie nini mama yako?”

“Ili niweze kushirikiana nanyi ninahitaji mama yangu mumpatie kiasi cha dila milioni kumi la sivyo sinto fanya chochote katika nchi yenu hata nikienda nchini Marekani, kwa maana raisi wangu ameamua ila na mimi nina maamuzi yangu kutokana kwangu”

Balozi akaka kimya huku akimtazama Adrus kwa maana kiasi cha pesa alicho kiomba hakikuwepo katika makubaliano na raisi Rahab.

“Ngoja niwasiliane na raisi wangu nchini Marekani?”

“Fanya hiyo na nitahitaji hiyo pesa kuingizwa kwenye akaunti ya mama yangu ndani ya hili lisaa moja kabla sijaondoka nchini Tanzania”

“Sawa”

Balozi wa Marekani akatoka katika chumba hicho, akatoa simu yake mfukoni na kumpigia raisi Dustan. Akamueleza vigezo na masharti ambavyo Adrus amevitoa, raisi Dustan hakuwa na kipingamizi zaidi ya kiidhinisha pesa hizo ili Adrus aweze kupatiwa. Balozi wa Marekani akarudi chumbani alipo Adrus.

“Wamakubali kuweza kufanya hivyo”

“Basi ninahitaji kuzungumza na mama yangu na kama ikiwezekana aletwe hapa Ikulu na kila kitu ninahitaji kifanyike hapa hapa ikulu hata nikiondoka basi ninaondola salama”

“Una simu hapo uwasiliane naye?”

“Ndio”

“Basi fanya hivyo”

Adrus akampigia mama yake simu, cha kumshukuru Mungu mama yake akaipokea mapema sana.

“Mama upo wapi?”

“Ndio ninatoka hapa Kariakoo”

“Basi subiri hapo hapo unakuja kuchukuliwa na kuletwa hapa ikulu”

“Ikulu, kuna nini tena”

“Utakuja kufahamu huku huku, baada ya dakika kadhaa utakuja kuchukuliwa ninakuomba usubirie hapo kwenye sheli ya big bon”

“Mmmmm sawa”

***

“Mume mfwatilia huyo kijana kwa sasa yupo wapi?”

Livna alimuuliza kijana wake anaye shuhulika na maswala ya mtandao.

“Ndio kuna mazungumzo haya hapa alikuwa akiwasiliana na mama yake ili aeleke ikulu”

Msicha huyo akamsikilizisha Livna mazungumzo hayo.

“Pia kuna mazungumzo ya balozi wa Marekani na raisi wake, amaidhinisha pesa ya kumkabidhi Adtrus ila sijafahamu ni kwa ajili gani?”

“Nina imani kwamba ataondoka nchini Tanzania, ndani ya muda mchache kuanzia hivi sasa. Hakikisheni kwamba unamfwatilia hadi uwanja wa ndege nina imani ndege aliyo ipanda itakuwa sehemu sahihi ya sisi kumpata sawa”

“Sawa mkuu”

“Andaa wasichana wenne waende kuitekeleza hiyo kazi”

“Sawa mkuu”

Livna baada ya kuzungumza hivyo akatoka chumbani humu, huku akiitazama meseji iliyo ingia muda mfupi ikiidhinisha pesa aliyo tumia na bwana Hamad Tariq kwa ajli ya kazi ya kumteka Adrus.

***

Dokta Benjamini akatoka katika chumba maalumu walicho kuwa wakimfanyia Eddy matibabu.

“Mume wangu anaendeleaje dokta?”

Phidaya aliuliza huku akiwa amejawa na shauku kubwa sana.

“Anaendelea vizuri baada ya masaa mawili hivi basi atazinduka”

“Ni nini kinacho msumbua?”

Rahab aliuliza kwa shauku kubwa.

“Ni mstuko ulio changiwa na hasira, umepekekea baadhi ya msipa kulete itilafu ndogo na kusababisha damu kumwagika puani, ila tumejitahidi kukabiliana na tatizo na atarudi katika hali yake ya kawaida.

“Ohooo asante Mungu”

Phidaya alizungumza huku akimbusu mwanye Camila shavuni.

“Kwa hiyo dokta unataka kuniambia hakuna tayizo jengine ambalo linaweza kumkabili mume wangu?”

Phidaya aliuliza kwa sauti ya upole huku akikmtazama dokta Benjamini.

“Hapana kwa kweli”

“Sawa, ninaweza kuingia kumuona”

“Ahaa manesi wanamaliza kumuweka sawa basi baada ya hapo mutaruhusiwa kumuona akizinduka”

“Sawa sawa”

Dokta Benjamini akaondoka katika eneo hilo, raisi Rahab akaitazama saa yake ya mkononi na kuona ni saa saba mchana.

“Jamani ninaomba niwakimbie kidogo, ila ulinzi utaimarisha vizuri na ninakwenda kulitangazia taifa juu ya kuumwa kwa makamu wa raisi ili watu waweze kumuombea”

“Sawa wifi yangu, ninakushukuru kwa kunijali mimi na familia yangu”

“Ni jukumu langu Phidaya, tumetoka mbali na tumefanya yaliyo mengi kwa pamoja hili ni jukumu letu”

“Asante sana”

Rahaba akambusu Phidaya shavuni mwake, akampungia mkono wa kumuaga Shamsa aliye kaa pembeni akionekana hana furaha kabisa. Raisi Rahab na walinzi wake wakarudi kwenye magari na kuondoka eneo hili la hospitalini huku wakiwaacha watu wakijiuliza maswali mengi kwani hawakutarajia kumuona raisi kwa wakati huo.

***

Mama Adrus akafikishwa ikulu huku akiwa haelewi ni kitu gani kinacho endelea, moja kwa moja akaingizwa katika chumba alipo Adrus.

“Mama”

Adru alizungumza huku akisimama, akampa mkono mama yake.

“Mbona sielewi elewi”

“Usijali nitakeelezea kila kitu”

Adru akamuelezea mama yake hali halisi iliyopo hivi sasa, pia akamueleza kiasi cha pesa ambacho mama yake ataingiziwa muda huu kwenye akaunti yake.

“Ina maana mwanangu ndio huto rudi tena?”

“Nitarudi mama yangu, usijali ni kazi ambayo sijui itakwisha lini”

“Sawa mimi sina tatizo, ila ninakuomba ujitunze mwanangu na hiyo pesa mimi nitakuwekea hadi pale utajapo rudi”

“Mama hiyo ni pesa nyingi sana ambayo hata ukiitumia wewe haiwezi kuisha leo wala kesho kutwa, cha kufanya nunua nyumba kubwa nyingine ile pale ikodishe, fungua miradhi mingi ili pesa iwe inazunguka sawa mama yangu”

“Saw animekuelewa mwanangu ila ninahitaji uwe makini”

“Nitakuwa makini mama na pia ninahakikisha nikirudi basi ninarudi na mke wako Naomi”

“Nitashukuru mwanangu, ila kama inawezekana murudi na mtoto”

“Hahahaaa sawa mama”

Mama Adrus akamkabidhi balozi wa Marekani namba ya akaunti yake ya benki. Kiasi cha dola milioni kumi kikaingiazwa kwenye akaunti yake kitu kilicho mfanya mama Adrus kusahau umasikini wake wote alio kuwa nao, na sasa furaha ya utajiri ikamjaa moyoni mwake. Wakaagana na mwanye kisha mama Adrus akaondoka ikulu huku moyoni mwake akidhamiria kwenda benki, kuchukau kiasi cha pesa na kununua gari zuri sana ambalo litamfanya aache kupanda dalalada.

***

Dokta Ranjiti kwa haraka akakurupuka kutoka kitandani kwake na kukaa kitako, akaichukua rimoti ya tv iliyopo kitandani mwake na kuisikiliza habari hii ya dharura.

‘Ninawaomba wananchi wote wa Tanzania kwa ujumla tuweze kumuombea makamu wetu wa raisi aweze kupata afya njema na kurudi katika majukumu yake ya kila siku. Mungu akapate kumtangulia katika kuirudisha afya yake asanteni”

Habari ikaisha hapo, kwa haraka dokta Ranjiti akashuka kitandani na kutoka chumbani kwake, akakutana na mlinzi wake akiwa naye anatoka chumbani kwake. Ikawalazimu wote wawili kurudi chumbani kwa dokta Ranjiti.

“Mume weza kufahamu huyu mshenzi ni wapi alipo lazwa?”

“Ndio mkuu, amelazwa katika hospitali ya Taifa Muhimbili na nina imani kwamba mke wake na mwanaye watakuwepo katika hilo eneo”

“Safi sana huu sasa ndio muda wa kwenda kumuua Eddy kwa mkono wangu mimi mwenyewe na ninamrudisha Phidaya wangu mikononi mwangu sasa.”

Dokta Ranjiti alizungumza huku akinyang’ata meno yake kwa nguvu, kwani kazi iliyopo mbele yake ni rahisi sana kwa yeye kuutekeza.


“Tafuteni usafiri wa kueleka Dar es Salaam sasa hivi”

“Sawa mkuu ila unaonaje tukakodi ndege ambayo itatupeleka moja kwa moja hadi Dar es Salaam?”

Doka Ranjiti akaka kimya huku akifikiria ushauri alio pewa na mlinzi wake.

“Sawa tafuteni ndege haraka tuondoke hapa Arusha”

***

Adrus akaingia kwenye gari maalumu kutoka ubalozi wa Marekani, moja akaelekea uwanaja wa ndege wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere akiongozana na balozi wa Marekani. Akakabidhiwa tiketi ya shirika la ndege la KLM.

“Utapokelewa uwanja wa ndege na sekretari wa Ikulu ya Marekani na utapelekwa moja kwa moja hadi Ikulu ya Marekani na kuanzia hapo kila kitu utaelekezwa huko”

“Shukrani sana”

Adrus alizungumza huku akimpa mkono balozi huyu wa Marekani. Adrus akaelekea katika eneo maalumu la kukaguliwa mizigo yake pamoja na hati yake ya kusafiria. Baada ya hatua hiyo akaelekea katika sehemu maalumu ya kuingilia katika ndege hiyo kubwa.

Wasichana wane walio valia mavazi ya wahudumu wa shirika la ndege la KLM, wakaingia ndani ya ndege hiyo na kuanza kuwapa maelekezo baadhi ya abiria ambao tayari wamesha ingia kwenye ndege yao akiwemo na Adrus.

Adrus akaka kwenye siti yake, taratibu akajifunga mkanda huku akimsalimia msichana aliye kaa naye pembeni yale. Abiria wote wakaingia kwenye ndege na kila mmoja akakaa kwenye siti inayo muhusu, abiri wakatangaziwa ndege hiyo kuondoka na kila mmoja ahakikishe kwamba anafunga mkanda wa siti yake.

“Ninaitwa Cookie”

Msichana huyo alizungumza huku akimtazama Adrus kwa macho yaliyo jaa uchangamfu mkubwa sana.

“Ninaitwa Adrus”

Adrus naye alijibu huku akimkabidhi mkono msichana huyu. Wakajikuta wakishikana mikono yao, wakisikilizia jinsi ndege hii inavyo anza kuacha ardhi na kupaa angani. Ndege ilivyo kaa sawa, wakaaachiana huku wakitazamana kwa macho ya kuiba iba.

“Samahani”

Adrus alizungumza huku akiwa amejawa na aibu kubwa kwani haitaji kuruhusu hisia za matamanio kuingia kwa msicha huyu ambaye ni mrembu sana.

“Bila samahani”

Cookie alizungumza huku akitabasamua.

***

“Mkuu hii kazi ninaweza kuifanya mimi peke yangu hakuna haya ya kwenda wengi”

Cookie alimuambia Livna huku akimtazama usoni mwake.

“Ila kumbuka kwamba mu anaye takiwa hapo ni hatari kwa jinsi ya maelezo yao, wewe utatumia njia gani kumnasa?”

Livna alizungumza huku akimtazama Cookie msicha aliye jaliwa kubarikiwa uzuri wa halisi. Shepu yake, uso wake na rangi ya mwili wake ambayo ni choclate, inawapagawisha wanaume wengi ambao wakimuona wanatokea kumpenda sana.

“Akili, unajua mtu kama hiyo hatutakiwi kumuendea kwa kasi, hatutakiwi kutumia nguvu kwa maana anaweza kutushinda na mwishowe sisi ndio tukaathirika katika hilo”

Wazo la Cookie likamfanya Livna kukubaliana naye.

“Basi hakikisha kwamba unaifanya hii kazi kabla muhusika hajafika nchini Marekani”

“Usijali muheshimiwa nitaifanya, wewe mwenyewe utafurahi”

“Basi inabidi kuwahi, tumia helicopter ikupeleke hadi Dar es Salaam na ndege aliyo katiwa tiketi Adrus imebakisha kama dakika arobaini na tano kuondoka”

“Sawa mkuu”

“Tiketi si ulisha katiwa?”

“Ndio nimekata kupitia mtandao. Cha kumshukuru Mungu, nimepata siti moja na huyo Adrus.”

“Safi, pesa utaingiziwa kwenye akaunti yako ya benki”

“Shukrani”

Cookie akaeleka moja kwa moja katika kiwanja kidogo cha helicopter kilicopo juu kabisa ya meli hii, akakuta rubani tayari amesha andaa helicopter hiyo, akaingia huku akiwa amebeba bagi lake dogo, wakaondoka eneo hili la baharini. Ndani ya dakika kumi waka tayari wamesha ingia katika jiji la Dar es Salaam. Wakatua maeneo ya karibu kabisa na kiwanja cha ndege. Cookie akashuka na kukodi pikipiki iliyo mpeleka moja kwa moja hadi kwenye kiwanja cha ndege, akafwata hatua zote ambazo zinatakiwa kufatwa, akaingia ndani ya ndege, na kukaa kwenye siti yake huku akishusha pumzi nyingi kwani amekimbizana na muda. Hazikupita hata dakika tano Adrus naye akaka kwenye siti ya pembeni yake.

‘Kazi imeanza sasa’

Cookie alizungumza huku akimtazama Adrus kwa furaha kubwa sana.

***

Wasi wasi mweingi ukamjaa Phidaya pamoja na Shamsa kwani masaa mawili ambayo waliahidiwa na daktari kwamba Eddy atazinduka, yamepita pasipo Eddy kuwa katika hali hiyo. Kupitia mlango wa kioo wa chumba alicho lazwa Eddy wakaendelea kuona jinsi mashine ya oksijeni inavyo fanya kazi.

“Sasa mbona aamki?”

Phidaya aliuliza huku machozi yakimlenga lenga usoni mwake. Shamsa hakujibu kitu chochote kwani akili yake inazidi kuchanganyikiwa kwa mambo mengi, ikiwemo kutekwa kwa manaye pamoja na rafiki yake Sa Yoo ambao hadi sasa hivi atambui ni wapi alipo na watu ambao alikuwa anawategemea ni Eddy na Adrus ambaye hadi sasa hivi haelewi Adrus yupo wapi.

“Shamsa nenda kamuite dokta”

Shamsa akaondoka eneo hilo, akauliza uliza kwa baadhi ya wauguzi na akaelekezwa ofisi ya dokta Benajamini kwa haraka Shamsa akaingia katika ofisi hiyo pasipo kubisha hodi na kuwafanya dokta Benjamini na mgeni aliye kuwemo humo ndani kustuka.

“Dokta ninakuhitaji hali ya baba yangu mbona haibadiliki?”

“Baba yako nani?”

“Dokta hunifahamu au, baba yangu ni makamu wa raisi, sasa nahitaji ukamuhudumie”

Dokta Benajamini kwa haraka akanyanyuka na moja kwa moja akaongozana na Shamsa hadi katika chumba alicho lazwa Eddy.

“Dokta mbona hanyanyuki tu masaa mawili yamesha pita?”

Phidaya alizungumza huku wasiwasi mwingi ukiwa umemjaa, dokta Benjamini akashusha pumzi huku akimtazama Eddy kwani kwa mawazo aliyo toka nayo ofisini kwake alihisi kwamba hali ya makamu wa raisi imekuwa mbaya.

“Hali yake itakaa sawa tu, kikubwa ninawaomba muwe wavimilivu katika hili”

“Tutakuwaje wavumilivu wakati ulituahidi masaa mawili?”

“Ndio nilizungumza hivyo ila kwa sindano ambayo tumemchoma inachukau masaa mawili au matatu, ninaomba tuendelee kuwa wavumilivu”

Dokta Benjamini alizungumza kwa sauti ya upole huku akimtazama Phidaya. Phidaya hakujibu kitu chochote zaidi ya kukaa kwenye kiti huku akiwa amemshikilai mwanye Camila. Dokta Benjamini akaingia katika chumba alicho lazwa Eddy, akazikagua mashine zinazo msaidia Eddya katika kupumu, alipo dhibitisha hakuna tatizo la aina yoyote akatoka.

“Nitarudi baada ya nusu saa kuangalia maendelo ya mgonjwa”

“Sawa”

Dokta Benjamini akawatazama walinzi wanne walipo katika eneo hili kisha akaondoka na kurudi ofisini kwake.

***

“Ninakwenda Marekani, kuchukua cheti changu cha chuo kikuu”

Cookie alizungumza kwa sauti nyororo huku akiyelegeza macho yake, yaliyo mfanya Adrus kutabasamu kidogo.

“Waooo vizuri sana”

“Asante, wewe ni Muislam?”

“Yaa ni Muislam kwa nini umeuliza dini yangu?”

“Ahaa ulivyo nitajia Adrus, nikahisi kabisa ni muislam ila nikaona ni vyema ni kuulize”

“Vipi wewe ni dini gani?”

“Mimi ni mkristo”

“Ila wakristo kwa sasa mumegawanyika katika madhehebu mengi mengi, labda wewe ni dhehebu gani?”

“Mimi ni Mkatoliki”

“Ahaaaa sawa sawa”

“Na wewe unakwenda Marekani kufanya nini?”

Adrus akaka kimya kwa sekunde kadhaa huku akitabasamu.

“Ninakwenda kwenye biashara zangu ndogo ndogo”

“Waooo, unafanya biashara gani?”

Cookie aliendelea kuwa mchangamfu sana kwa Adrus, na kuzidi kumsogeza Adrus karibu yake kihisia kwa maana anatambua uzuri wake ndio ngao yake.

“Aha…ninachukua simu hizi aina ya Iphone, ninakwenda kuziuza dukani kwangu Tanzania”

Adrus ilimbidi kudanganya pasipo kujua kwamba Cookie anafahamu kila kitu juu yake na hata anayo yazungumza yote ni uongo.

“Alafu hiyo biashara inalipa kweli kwa maana mimi tangu nimemaliza chuo nilikaa kaa tu nyumbani nikisubiri majibu yangu ya chuo?”

“Unalipa pale unapo kuwa na wateja wa kutosha na umaarufu”

“Kwa hiyo unataka kuniambai kwamba ni kiasi gani cha pesa ambacho kama nikihitaji kuingia kitatosha?”

“Ukiwa na milioni zako ishirini basi unapiga kazi vizuri tu, so ikukulipa mtaji unaweza kuwa hadi milioni mia, mia mbili au mia tatu”

“Duuuu kweli, na wateja Tanzania wapo?”

“Wapo wengi sana, tazama hata wewe hapo si umeshika iphone?”

Cookie akaitazama simu yake na kuangua kicheko kidogo.

“Yaa ujue wateja ndio nyinyi”

“Kweli, unajua hizi simu ni nzuri sana, na mimi nina zipenda kwa kweli. SasaTanzania unarudi lini?”

“Ahaa ndani ya wiki ijayo nitageuza, sinto kaa sana”

“Habari zenu?”

Muhudumu alizungumza huku akiwatazama Adrus na Cookie.

“Salama habari ya wewe”

Cookie alijibu kwa furaha.

“Salama, niwaletee vinywaji gani?”

“Mimi ninaomba maji tu.”

“Basi na mimi ninaomba maji kama alivyo zungumza kaka yangu hapa”

“Sawa”

Muhudumu huyu akaondoka na kuwaacha Adrus na Cookie wakitazamana. Wakajikuta wakitabasamu kwa pamoja huku kila mmoja akiangali pembeni.

‘Ila sihitaji kumsaliti Naomi wangu’

Adrus alizungumza kimoyo moyo huku akijikaza kuzuia msisimko wa mapenzi ulio mvamia katika moyo wake.

“Una mchumba?”

Swali la Cookie likamstua sana Adrus, taratibu akazibana pumzi zake na kuzishusha kwa utaratibu ulio mfanya Cookie aanze kufahamu udhaifu wake.

“Ohooo samahani kama nitakuwa nimekuudhi”

Cookie alijiahimi huku akimtazama Adrus usoni mwake.

“Aha…hapana usijali. Ila ninaye”

“Sawa sawa”

“Vipi kwa upande wako?”

“Ahaa msema kweli ni mpenzi wa Mungu, nilikuwa naye ila kwa bahati mbaya tumeachana”

“Why?”

“Tabia zake sikupendezeshwa nazo alikuwa mgomvi, mlevi ana penda disko. Ukienda naye disko anakutelekeza anakuwa na wanawake wengine. Kusema kweli nikaona hanifai na si mwanaume ambaye nilikuwa nina muhitaji”

Muhudumu akawaletea chupa za maji, Adrus akazipokea zote mbili kisha akamkabidhi Cookie na yeye.

“Asante”

Adrus alimuambia muhudumu aliye wakabidhi chupa hizo za maji.

“Wewe unapenda mwanaume wa aina gani?”

“Ahaa napenda mwanaume, mpole, anaye jali, anaye jitambua anatakiwa kuwa na jukumu gani kwa mpenzi wake. Mwanaume mwenye kujua nini maana ya mwanamke.”

“Waooo ni chaguzi zuri kweli hilo”

“Yaaa awe mcha Mungu pia, kwa maana akiwa si mcha Mungu ninajua siwezi kuipata amani ya moyo wangu”

“Kweli, hapo unatakiwa upate mlokole mmoja safi kabisaaa”

“Hahahaaa….hapana kwa kweli, sihitaji yule ambaye amepitiliza hata kwenye mambo fulani analeta ulokole”

“Mambo gani?”

Adrus aliuliza huku akitabasamu jambo lililo mfanya Cookie kuzidi kucheka.

“Mambo yake”

“Yale yapi si uzungumze”

“Hahahaaaa, Adrus wewe sio mtoto bwana”

Mazoe ya muda mfupi yakajenga furaha kubwa sana yao, Cookie japo kwa ajili ya kumdhuru Adrus ila akajikuta akianza kuipinga roho yake mbaya ya kishetani. Akamtazama Adrus ambaye ni kijana bado mdogo, kijana mwenye uzuri wa kipekee, kiaja mchangamfu. Kijana mwenye kila sifa ambayo kwenye maisha yake anatamani sana kumpata mwanaume wa aina hiyo ila kazi na malenzi aliyo kulia hayamruhusu kufanya hivyo.

‘Adrus siwezi kukufanyia unyama, lazima uwe wangu, lazima nikusaidie kaifanya hii kazi iliyopo mbele yako’

Cookie alizungumza huku akimtazama Adrus jinsi anavyo kunywa maji yaliyomo kwenye chupa, kitendo cha Adrus kuitoa chupa mdomoni mwake, taratibu Cookie akausogeza mdomo wake karibu kabisa na lipsi za Adrus na kumfanya Adrus kutetemeka mwili mzima kwani kwenye maisha yake hajatarajia kuchepuka siku hata moja na Naomi ndio mwanake wake wa kwanza kwenye maisha yake tangu alivyotoka tumboni mwa mama yake.



Cookie akashindwa kuurudisha mdomo wake nyuma na kujikuta akiigusanisha midomo yake na midomo ya Adru ambaye anahema kwa pumzi za wago. Taratibu Cookie akupenyeza ulimi wake katika midomo ya Adrus na kumfany Adrus aishiwe nguvu kabisa. Cookie hakujali watu walipo katika siti za pembeni, alipi jirishisha na unyonaji wa midomo ya Adrus akamuachia taratubu huku macho yakimlegea.

“Adrus samahani”

Cookie alizungumza kwa sauti ya unyonge huku akikaa vizuri kwenye siti yake. Adrus akajikuta akishindwa hata kufumbua kinywa chake kwani alicho fanyiwa ni Cookie, kimegusa udhaifu wake ambao siku zote anashindwa kuuhimili pale anapo kuwa na mwanamke.

***

Dokta Ranjiti na walinzi wake wakafanikiwa kupata ndege ya kukodisha, kwa haraka wakaanza safari ya kuelekea jijini Dar es Salaam lengo lake ni kuhakikisha kwamba anamteketeza Eddy na kumpata Phidaya. Kwa jinsi ndege inavyo kwenda akahisi hata rubani anaiendesha taratibu.

“Waambie waende kasi”

“Mkuu mbona tupo kasi”

Mlinzi wa dokta Ranjiti alizungumza huku akimtazama bosi wake huyu.

“Natamani tufike sasa hivi nikamuangamize huyu mshenzi”

“Usijali mkuu tutafika na tunatakiwa kuwa makini na nina amini kwamba Muhimbili lazima ulinzi utakuwa ni mkali sana”

“Ahaaa mimi nitaingia kama daktari na kazi hiyo nitaifanya mimi mwenyewe na nitahitaji munisubirie nje”

Walinzi hawa wakatazamana kwani maamuzi aliyo yatoa mkuu wao yanawashangaza sana.

“Lazima nimue, lazima afe”

Dokta Ranjiti alizungumza kwa msisitizo mkubwa, kiasi cha kuwashangaza hadi walinzi wake ambao hawaelewi kuna tatizo gani lilipo kati ya bosi wao na makamu wa raisi bwana Eddy Godwin.

***

“Siwezi kuendelea kuwa mjinga”

Sa Yoo alizungumza kwa sauti ya chini huku akimtazama mlizi wa kiume aliye achwa naye humu ndani.

“Nahitaji maji”

Sa Yoo alizungumza huku akimtazama mlinzi huyu. Taratibu mlinzi huyu akafunga friji dogo lililomo humu ndani ya chumba hichi walicho muweka Sa Yoo, akamimina kiasi cha maji kwenye glasi na kumsogelea Sa Yoo.

“Sasa nitakunywaje maji nikiwa mumenifunga kamba”

Mlinzi huyu akamtazama Sa Yoo, kujiamini kwake kwa kuwa na silaha, akatoa kisu kidogo kwenye mfuko wa suruali yake, kosa kubwa ambalo atalijitua katika maisha yake ni kukata kamba ya mkono wa kulia wa Sa Yoo.

Sa Yoo kwa haraka akaitumia nafasi hiyo kumpiga mlinzi hiyo kwenye maeneo ya siri na kumfanya aanguke chini huku akiugulia maumivu ya eneo hilo ambalo mwanaume yoyote endapo atapigwa hapo, hata kama ni mbabe kiasi gani lazima ajikunje kwa maumivu. Kwa haraka Sa Yoo akajisogeza kipo agukia kisu alicho kuwa amekishika mlinzi huyu akakiokota, akakata kamba zate alizo fungwa katika mkono wake wa kushoto pamoja na miguuni. Akaichukua bastola ya mlinzi huyu, akatoa magazine na kukuta ina risasi za kutosha, akairudisha na kujichomea kiunoni mwake, akampapasa na kukuta funguo za mlango wa kutokea humu ndani pamoja na simu. Akazichukua kwa pamoja, akampiga teke la kichwa mlinzi huyu na kumfanya apoteze fahamu.

Kwa haraka Sa Yoo akakimbilia hadi dirishani akachungulia nje na kuona hakuna mtu yoyote anaye weza kuja eneo hili. Sa Yoo akatazama kama kuna salio la kutoka katika simu hiyo, kwa bahati nzuri akakuta salio la kutosha.

Akaingiza namba ya Shamsa na kumpigia, cha kushukuru Mungu simu ya Shamsa ikaanza kuita baada ya sekunde kadhaa ikapokelewa.

***

Mawazo mengi yakaendelea kukitesa kichwa cha Shamsa, akamtazama Phidaya na mwanaye walio kaa pembeni yake, taratibu akanyanyuka, akasimama kwenye mlango wa kioo unao onyesha kila kitu ndani ya chumba alicho lazwa Eddy, taratibu akashusha pumzi nyingi huku akijaribu kufikiria ni kitu gani anaweza kukifanya. Mlio wa simu yake ukawastua hadi walinzi walio simama katika eneo hilo, kwa haraka Shamsa akaanza kutembea kuondoka katika eneo hilo ambalo halitakiwa kielele zozote, akaitoa simu yake mfukoni na kukuta namba mpya kutoka nchini Uingereza, moyo ukamstuka, ila akajikaza na kuipokea simu hiyo.

“Halooo”

“Shamsa ni mimi Sa Yoo”

“Sa Yoo…..!!!”

“Ndio naomba unisikilize, hapa nilipo sifahamu ni wapi, ninacho kuomba uweze kuwasiliana na kikosi chochote cha usalama uwatumie hii namba yangu waitafute na kujua ni wapi nilipo”

“Sawa nitafanya hivyo, mwanangu yupo wapi?”

“Ameondoka naye John kwa hiyo sijui hata yupo wapi kwa kweli”

“Ohoo Mungu wangu”

“Samahani sana rafiki yangu, ila nitajitaidi kumukoa Junion Jr sawa”

“Nakuomba ufanye hivyo rafiki yangu, ngoja nizungumze na……..ok nafanya hivyo sasa hivi naomba usizime si…..”

Shamsa akastushwa na milio ya risasi iliyo sikika upande wa pili wa simu na kumfanya aanze kuita Sa Yoo kwa mara kadhaa ila hakuweza kujibiwa chochote jambo lililo mchanganya sana.

Sa Yoo kwa haraka akarudi hadi eneo la chumba, akamshika mlinzi mmoja mkono na kumsogeza pembeni.

“Vipi dada nikusaidie nini?”

“Nahitaji…..nahitaji……uuong….ee na raisi”

Shamsa alizungumza kwa kigugumizi kikali kilicho mfanya mlinzi huyu kushangaa. Phidaya taratibu akanyanyuka huku akiwa amembeba Camila. Akasoge hadi eneo ambalo Shamsa amesimama na mlinzi huyo.

“Shamsa kuna nini?”

Phidaya alizungumza kwa unyonge.

“Nahitaji kuzungumza na raisi”

“Kuna nini kinacho endelea?”

“Mama elewa tu nahitaji kuzungumza na raisi”

Phidaya hakuwa na kipingamizi, akaitafuta namba yaRahab na kumpigia, simu ya Rahab ikaita kwa muda kisha ikapokelewa. Phidaya hakuzungumza chochote zaidi ya kumkabidhi Shamsa. Shamsa akaipokea kwa haraka akasogea pembeni eneo ambalo hakuna mtu ambaye anaweza kuyasikia mazungumzo yake.

“Haloo wifi mbona uzungumzi”

“Ni mimi”

“Shamsa!!?”

“Ndio, unahitaji kufahamu ni kitu gani kimepekea Eddy akawa katika hali aliyo kuwa nayo hivi sasa?”

“Ndio niambie”

Raisi Rahab aliuliza kwa shauku kubwa sana.

“Ni hivi, Eddy na mimi tuna mtoto wa kumzaa, anaitwa Junion Jr hadi sasa hivi ninavyo zungumza ni kwamba mtoto huyo ametekwa na John nchini Uingereza na Sa Yoo naye ametekwa na John huyo, sasa ninaomba msaada wako, ili uweze kumsaidia Eddy arudi kwenye hali yake ni lazima mwanaye aweze kuwa salama, alimkabidhi Adrus kazi hiyo ila wewe ukabadilisha makubaliano ndio maana Eddy alihitaji kuifanya hiyo kazi peke yake”

Shamsa alizunumza kwa haraka sana kiasi cha kumfanya raisi Rahab kushusha pumzi nyingi sana kwani anacho kisikia sasa hivi ni jambo jipya kabisa.

“So utanisaidia au hauto nisaidia?”

“Umezungumza na Sa Yoo?”

“Nimezungumza naye hivi sasa hivi”

“Nitumie namba aliyo itumia”

“Sawa”

Shamsa kwa haraka akakata simu na kuinakili namba aliyo itumia Sa Yoo katika simu ake upande wa meseji, alipo hakikisha kwamba ameinakili. Akamtumia raisi Rahab, kisha akarudi katika eneo alipo Phidaya na walinzi huku macho yakiwa yamejaa uwekundu wa hasira hadi rangi ya mwili maeneo ya pua yakabadilika na kutawaliwa na uwekundu fulani hivi.

“Shamsa kuna nini kinacho endelea”

“Hakuna kitu”

Shamsa alizungumza kwa sauti iliyo jaa mikwaruzo huku akimkabidhi Phidaya simu yake na akarudi katika kiti alicho kuwa amekaa, jambo lililo mshangaza Phidaya ambaye haelewi chanzo ni nini hadi Shamsa kukasirika kwa kiasi hicho.

***

Rahaba akajikuta aiishiwa hata hamu ya kufanya kazi ambayo alikuwa anaipitia pitia, akaitazama meseji aliyo tumia kutoka kwa Shamsa.

‘….Eddy na mimi tuna mtoto wa kumzaa, anaitwa Junion Jr…..’

Kauli hii ikajirudia tena kichwani mwa Rahab na kujikuta moyo wake ukitawaliwa na maumivu makali sana.

‘Shamsa na Eddy wamezaa mtoto…..hapana huyu binti amechanganyikiwa kwa kweli’

Rahab alizungumza ili kujipa moyo kwa maana na yeye moyo wake wote amekabidhi Eddy na amekubaliana na mahusiono ya Eddy kuwa na Phidaya kwa maana amemkuta, ila kwa Shamsa ni jambo jengine la kumshangaza sana. Taratibu Rahab akampigia simu sekretari wake na kumuomba aingie ofisini kwake. Sekretari akaingia ofisini humo na kusimama mbele ya meza ya raisi Rahab.

“Wasiliana na waziri mkuu wa Uingereza”

“Sawa”

Sekretari huyu akatoka na kumfanya Rahaba agemee kiti chake huku akiwa amechoka sana.

‘Eddy amezaa kweli na Shamsa…..haiwezekani haaaaa hapana kwa kweli’

Raisi Rahab aliendelea kujipa matumani moyoni mwake, simu ya mezani mwake ikamstua, akaipokea na kuweka loud speaker.

“Muheshimiwa waziri mkuu yupo kwenye line namba moja unaweza kupokea”

Rahab akafwata maelekezo ya sekretari wake, akaminya batani namba moja iliyopo katika simu hii ya kisasa ya mezani.

“Madama Raisi habari yako”

“Salama waziri mkuu, nashukuru sana kwa kukubali wito wangu wa kuzungumza nami”

“Usijali madama raisi, sisi ni marafiki wa kipindi kirefu”

“Kweli, sasa muheshimiwa waziri mkuu ninakuomba unisaidie jambo moja, kuna kijana wangu mmoja ametekwa katika nchi yako, amebahatika kupata simu ya mkononi na hapa amempigia mmoja wa rafika yake hapa nchini Tanzania, ninakuomba nikutajie namba ambayo unaweza kunisaidia kutafuta eneo hilo na mukanisaidia kumtafuta”

“Ohoo sawa ninakuomba unitajie”

Raisi Rahab akaanza kumtaji waziri mkuu wa Uingereza namba hiyo aliyo tumiwa na Shamsa.

“Nimeipata, ngoja niiikabidhishe katika vikosi vya usalama sasa hivi na kazi inaanza kufanyika haraka sana”

“Sawa, je ninaweza kuona oparesheni hiyo itakavyo endeshwa?”

“Ngoja niwasiliane na mkuu wa jeshi la nchi kavu, baada ya hapo nitawasiliana na wewe baada ya kuweza kupata eneo maalumu ambalo muhusika yupo je, kijana wako ni mwanaume au mwanamke?”

“Ni mwanaume anaitwa Sa Yoo ana asili ya Kikorea, ana mcho makubwa kiasi na ni mwembamba”

“Nashukuru baada ya dakika kumi tutawasiliana madam raisi”

“Nashukuru muheshimiwa raisi”

Rahab akakata simu huku akiwajaribu kuanza kuvuta hisia kwa kile alocho kisikia kwa Shamsa je ni kweli. Uwezo wake wa kuvuta hisia haukuweza kwenda mbali na kujikuta kichwa kikumuuma sana kiasi cha kuanza kuhisi kizunguzungu.

***

Dokta Ranjiti na walinzi wake wafika uwanja wa ndege, wakatoka katika kiwanja hichi, wakakodisha teksi, na kumpa dereva maelekezo awapeleke katika hospitali ya Muhimbili. Dokta Ranjiti akaangali saa yake ya mkononi na inamuonyes hivi sasa ni saa tisa alasiri.

“Mkuu labda ni kwa nini umepania sana kufanya kile kinacho tupeleka huko?”

Mlinzi mmoja aliuliza kwa mafumbo ili kumficha dereva taksi asielewe ni kitu gani kinacho zungumziwa na watu hao.

“Amenichukulia mke wangu, na isitoshe amemzalisha kabisa na mtoto hata kama ni wewe hapo utajisikiaje?”

Dokta Benjamini alizungumza huku machozi yakimlenga lenga usoni mwake. Laiti walinzi wake wangefahamu ukweli kwamba Dokta Ranjiti ndio mwizi wa mke na alijaribu kumchoma sindano Phidaya ya kupoteza kumbukumbu wala asinge zungumza uongo wa aina hiyo.

“Mmmm, mke anaume mzee wangu”

Dereva taksi naye alijikuta akiripoka kama mada inayo zungumziwa hapo ina muhusu.

“Sasa mkuu hapo inabidi itumike akili, tena akili kubwa sana unafahamu mtu mwenyewe ni hatari sana”

“Sijali katika hilo kikubwa ni kuhakikisha ninamrudisha mke wangu mikononi mwangu”

“Mkuu ninacho kushauri katika hili tutumie akili, nguvu haitakiwi. Natambua una hasira kali sana ila ninakuomba tutumie akili sana”

“Sahamani jamani kwa kuwaingilia mazungumzo yenu, mzee ni nani aliye kuibia mke wako huyo na nimtu hatari?”

“Na wewe hayakuhusu fanya kazi yako umbea sitaki mimi”

Dokta Ranjiti alizungumza kwa kufoka sana, hadi dereva akajikuta akiogopa.

“Ila mkuu kijana anaweza kutusaidia”

“Ndio maana niliwaambia hii kazi nitaifanya mimi peke yangu na nitawaacha getini na sihitaji kuingia na mtu yoyote ndani ya hospitali.

Dokta Ranjiti akaendelea kuusimima msimamo wake, walinzi wake hawakuna na jinsi ya kufanya ukitegemea tajiri wao haambiliki wala hashauriki katika kuamua maamuzi yake. Wakafanikiwa kufika katika hospitali ya Taifa, Muhimbili.

“Nisubirini humu ndani?”

Dokta Ranjiti alizungumza huku akifunga mlango wa gari na akashuka, walinzi wake wakabaki ndani ya gari huku wakimtazama bosi wao jinsi anavyo pogoma kuingia ndani ya hiyo hospitali. Dokta Ranjiti kutokana anaitambua hospitali hiyo vizuri, moja kwa moja akaelekea katika chumba cha kuhifadhia nguo za madaktari, akachukua jaketi moja jeupe, akalivaa vizuri. Akachukua kitambaa cheupe kama madaktari wanao ingia katika chumba cha upasuaji, akavaa gloves nyeupe mikononi mwake, kisha akatoka katika chumba hichi. Hapakuwa na mtu aliye mstukia kwa maana katika hospitali hii kuna watumishi wengi sana, na hata madaktari wa kiarabu wapo wengi, kwa hiyo ni ngumu sana kwa mtu kumuuliza dokta Ranjiti anafanya nini katika eneo la hospitalini hapo. Dokta Ranjiti akatembea hadi katika eneo la mapokezi.

“Makamu wa raisi amelezwa wodi gani?”

Dokta Ranjiti alimuuliza nesi aliyopo hapa mapokezi, nesi akamuelekeza wodi wambayo makamu wa raisi Eddy Godwin amelazwa. Dokta Ranjiti akaondoka eneo hili huku akitabasamu, akajifunga kitambaa chake usoni mwake akiamini kwa kutumia njia hiyo itakuwa ni rahisi sana kumuua Eddy kwani kwa kujifunga kitambaa hicho si rahisi kwa mtu yoyote kuweza kumstukia hata kama akimkuta Phidaya katika eneo la chumba hichi alicho elekezwa.



Dokta Ranjiti akazidi kusonge mbele huku akijiamini sana, akafanikiwa kufika eneo la karibu kabisa na wodi aliyo kuwa amelekezwa, kitendo cha kumuona Phidaya akiwa amebeba mtoto mikononi mwake, kikamfanya ajawe na wasiwasi mwingi sana, akajaribu kupiga hatua moja mbele ila akamuona Shamsa akiwa amesimama akionekana kama mtu mwenye mawazo mwengi. Akawatazama walinzi hawa wa makamu wa raisi, kila mlinzi anaonekana kuwa makini sana na kila mtu anayelisogelea eneo hili.

‘Pumbavu sana’

Dokta Ranjiti alizungumza huku akigeuka na kurudi alipo toka, akakunja kona kwenye moja ya kordo, akatoa simu yake mfukoni, akaitafuta namba ya mmoja wa walinzi wake kisha akampigia. Simu ya mlinzi wake huyo ikaita kwa mara kadhaa ila haikupokelewa jambo lililo mfanya dokta Ranjiti kukasirika kwa maana hapendi ujinga akiwa katia eneo la kazi tena kwa kazi hii kubwa iliyo mleta hapa nchini Tanzania.

“Chizi wewe pokea simu”

Dokta Ranjiti alizungumza kwa hasira huku akivua kitambaa alicho jifunga usoni mwake. Akiwa katika hii kordo ambayo ipo juu ya goroa, akaona kundi kubwa la watu wakiwa wamekusanyika katika maeneo ya gatini, taratibu akasogelea dirisha na kuchungulia ili kuweza kujua ni kitu gani kinacho endelea, akaone kontena kubwa likiwa limeanguka, huku watu wakionekana kufanya jitihata za kulinyanyua, pembeni eneo lilipo anguka kontena hilo kuna gari kubwa aina Scania. Dokta Ranjiti akapiga hatua mbili mbele huku akifikiria nini cha kufanya ili afanikiwe kuingia katika wodi aliyo lazwa Eddy, ila moyo wake ukahisi kitu na kumfanya arudi tena dirishani kuangalia mkusanyiko huo mkubwa wa watu. Mapigo ya moyo yakaanza kumuenda mbio baada ya kugundua eneo lilipo angukia kontena pembeni yake ndipo kulipokuwa na taksi ambayo aliwaacha walinzi wake pamoja na dereva.

“Shitt”

Dokta Ranjiti alizungumza huku akitoka kasi na kueleeka katika eneo hilo la ajali ili akihitaji kudhibitisha kama kweli vijana wake ndio wameangukiwa na kontena hilo au sivyo. Hakuchukua muda hata wa dakika nne akawa amesha fika eneo la tukio, macho yakaomtoka alipo ona taksi hiyo ikiwa imebondwam na watu walio kusanyika wanadai kwamba ndani ya hilo gari lililo angukiwa kuna watu wawili walio kaa siti za nyuma

****

Kukimbia kimbiwa kwa madokta na manesi katika kordo iliyopo kwa mbali kidogo kimshangaza Shamsa na Phidaya ambao wote wanatamani kujua ni kitu gani kinacho endelea kwa maana hali ilikuwa shwari kabisa.

“Kuna nini?”

Shamsa alizungumza huku akimtazama mmlinzi mmoja.

“Kaa chini dada ninakwenda kuangali ni kitu gani kinacho endelea”

“Au hospitali imevamiwa?”

Phidaya alizungumza kwa shauku kubwa huku akinyanyuka yeye na mwanaye.

“Mom, tunakuomba ubaki hapa”

Walinzi wengine walinzungumza huku wakimuangalia mlinzi mmoja akiondoka katika eneo hili huku akiwa ameshika bastola mkononi. Shamsa akamtazama Phidaya ambaye macho yamemtoka, kifua kinamnynyuka kwa haraka ikiashiria kwamba mapigo yake ya moyo yanakwenda kasi sana. Shamsa akaanza kuondoka eneo hilo japo walinziw alijaribu kumzuia ila akawashinda ujanja na kukimbilia eneo ambalo anaona watu wanakimbilia.

“Nesi kuna nini kinacho endelea?”

“Kuna ajali imetoke hapo nje ya geti”

“Ajali ya nini?”

“Kuna contena limeangukia katika gari ndogo”

Nesi alizugumza huku jasho likimwagika akionekana na yeye amatoka katika eneo hilo la ajali. Shamsa wala hakumuaga daktari nesi huyo baada ya kupewa malezo hayo. Akajumuika katika kundi kubwa la watu wanao endelea kufanya kila liwezekanalo kujaribu kuonyanyua kontena hilo.

“Madam unatakiwa kurudi ndani hili eneo sio salama”

Mlinzi alizungu huku akimshika mkono Shamsa.

“Ngoja kwanza”

Shamsa alizungumza huku akimtazama mwanaume aliye valia koti jeupe la kidaktari, kichwa cha mwanaume huyu kwake sio kigeni kabisa. Ni kichwa ambacho anakifahamu vizuri hata akikitazama kwa nyuma.

“Madam”

“Ngoja”

Shamsa alizungumza kwa ukali huku akizidi kujipenyeza katikati ya watu kumfikia mwanaume huyo aliye simama mbele kabisa ya kundi hili la watu akishangaa gari ilivyo pondeka. Shamsa akamkaribi, kwa haraka akamshika mkono, kama hisia za akili zake zilivyo kuwa zimemuelekeza ndivyo jinsi zilovyo dhibitisha kwamba huyo aliye mshika ni dokta Ranjiti adui wanaye pambana naye kwa kupindi kirefu kuhakikisha kwamba wanamkamata. Dokta Ranjiti macho yakamtoka alipo muona Shamsa amesimama pembeni yake huku sura yake ikiwa imejawa na hasira kali sana.

“Do you miss me?”

Shamsa alizungumza kwa msisitizo huku akiendelea kuung’ang’ania mkono wa dokta Ranjiti aliye tamani hata dunia ipasuke imeze kwani amejiingiza katika mtu ambaye hana huruma kabisa, na anafahamu timbwili timbiwili la Shamsa vizuri sana.

***

Mwili mzima wa Sa Yoo ukaanza kumtetemeka baada ya kufyatua risasi kadhaa kwa mlinzi aliye kuwa akijaribu kunyanyuka ili amshambulie. Macho yakamtoka huku akiitazama simu iliyo mponyoka mikononi mwake wakati alipo kuwa anajaribu kumdhibiti mlinzi huyu. Kwa Haraka Sa Yoo akaanza kuiokota simu hiyo iliyo toka bretri pamoja na mfuniko wake. Kwa haraka akairudisha betrii ya simu katika sehemu husika, akaufunga mfuniko wa simu haraka. Akajaribu kuiwesha ila haikuwaka, akarudia mara kadhaa kuminya batani ya pembei ya simu hiyo ila haikuweza kuwaka. Sa Yoo akachungulia dirishani na kuona gari mbili nyeusi zikisimama kwa haraka katika eneo hilo.

‘Ooohoo Mungu wangu’

Sa Yoo alizungumza kwa kuchoka, baada ya kumuona Kimbery na vijana wake wakishuka katika gari hizo wakiwa na bunduki. Akili ya Sa Yoo ikaanza kufanya kazi kwa haraka kama computer huku akifikiria ni kitu gani afanye ndani ya chumba hichi kilicho hifadhiwa vitu vingi sana. Sa Yoo akautazama mlango wa chuma unao ingilia katika hichi chumba. Kutokana umefungwa kwa ndani, akaamini kwamba hadi Kimbery na watu wake waingie ndani humo itawachukua muda mrefu sana.

Sa Yoo akaanz akuzunguka ndani ya chumba hichi huku akitafuta jisni ya kutoka huku mlangoni akisikilizia jinsi unavyo bondwa kwa kitu kizito ili ufunguke. Kwa habati nzuri Sa Yoo akaona sehemu ya chini iliyo funikwa na mfuniko wa chuma, akalishika kufuli lililo ifunga sehemu hiyo, akaanza kulipiga piga kwa kitako cha bunduki ila kufuli halikufunguka. Sa Yoo kwa haraka akasimama na kurudi nyuma, akafumba jicho leke moja huku akiwa ameishika bastola kwa mikono yake miwili. Akabana pumzi yake, kisha akafyatua risasa mbili zilizo pelekea kufuli hilo kuvunjika, kwa haraka akasogea katika eneoe hili akaufungua mfuniko huo na kukuta ngazi za chuma zinazo eleleka chini, mwanga hafifu unao onekana katika hilo eneo ukamfanya ajiamini na kuingia ndani humo. Akaanza kushuka kwa harak katika ngazi hizo, kitendo cha kuingia chini. Kimbery na watu wake wanafanikiwa kuufungua mlango huo.

“Kagueni eneo zima”

Kimbery alizungumza mara baada ya kuona kiti alicho kuwa amekalia Sa Yoo hakina kitu chochote, mlinzi aliye kuwa amempa jukumu la ka kumlinda Sa Yoo, amelala chini huku damu zikimtoka mwilini mwake.

‘Malaya mkubwa’

Kimbery alizungumza kimoyo moyo huku akiwa amefura kwa hasira kali sana kwani jukumu la kuendelea kumshikilia Sa Yoo ni la kwake, na endapo mkuu wake John akifhamu kutoweka kwa Sa Yoo basi inaweza kupelekea kupewa hata adhabu ya kifo.

“Mkuu”

Kijana mmoja wa Kimbery aliita na kwa ishara akamuonyesha Kimbery aneo ambalo Sa Yoo amelitumia kwa ajili ya kutorokea katika eneo hilo.

“Sote tunakwenda chini”

Kimbery alizungumza kwa msisitizo huku akiwatazama vijana wake hawa wanao fwata kila amari ambayo anaizungumza mbele yao.

***

“Praaaaaaa…….tara….tararriraaaaa”

John alifanya vituko mbele ya Junion Jr huku akimshika mashavu yake. Japo ana roho ya kikatili sana, ila bado moyoni mwake hajafikiria kumuua mtoto huyu wa Eddy, ambaye amazaa na Shamsa. Simu yake ikaanza kuita na kumfanya kukatisha michezo yake na Junion Jr ambaye kwa muda mchache ametokea kumzoea John. Akaitoa simu yake mfukoni na kukuta ni namba ya waziri mkuu wa Uingereza, akaitazama kwa sekunde kadhaa kisha akaipokea.

“Habari yako mkuu John”

“Salama waziri, mbona saa hizi kuna nini kinacho endelea?”

“Raisi wa Tanzania, Rahab ameamua kuanzisha vita na wewe”

John akastuka sana, akamtazama Junion Jr, kisha akaanza kutembea hatua hadi dirishani mwa jumba lake hili lililopo katika kisiwa hichia anacho kimiliki kwa sasa.

“Vita gani?”

“Kuna binti ambye umemshikilia na yupo kwenye kisiwa chako, binti huyo anatafutwa na serikali ya Tanzania, hadi sasa ninavyo zungumza balonzi wa nchini Tanzania hapa Uingereza yupo njiani kufika hapa ofisini kwangu, na raisi Rahab ameomba kuishuhudia oparesheni ya kuvuania eneo lako moja kwa moja akiwa nchini kwake Tanzania”

“Huyu malaayaaaaaaaaaaaaaaaa………………”

John alizungumza kwa hasira sana.

“Hakikisha unafanya kitu kuendelea kuulinda umoja wetu la sivyo D.F.E inakwenda kuangamia leo”

Simu ikakatwa na kumfanya Jonh kushika moja ya pambo la maua lililopo pembeni yake na kuliangusha chini kwa nguvu. Mlio wa vvunjiko wa chombo hicho cha dongo kilicho kuwa kimewekea uwa hilo, kikawafanya walinzi wawiliwa John kuingia ndani ya chumba chake cha kulala ili kuweza kujua ni kitu gani kimetokea kwa bosi wao.

“Waataarifuni wanajeshi kwamba kila kikosi chochote cha askari kitakacho ingia hapa kisiwani, iwe boti au meli wahakikishe wana kitungua sawa”

“Sawa mkuu”

John akatembea kwa haraka hadi kwenye kabati lake la nguo, akatoa koti lake kubwa njeusi linalo karibia mfika chini pale anapo lifaa, akatoa kofiia nyeusi, zinazo julikana kama Cowboy, akaivaa kichwani mwake, kisha akalivaa koti hilo. Akamsogela Junion Jr aliye kuwa amemlaza kitandani mwake, akambeba na kuanza kutoka naye. Moja kwa moja wakaekelea katika manohari kubwa ya dharura iliyopo pembezoni mwa kisiwa hichi, akaingia na walinzi wake kadhaa, kisha taratibu manuwahi hiyo ya kivita ikaanza kuzama ndani ya maji na kuondoka eneo hilo kabisa.

***

Rahab akajikaza na kunyanya kwenye kiti chake alicho kikalia, akatoka nje ya ofisi yake na kuwakuta walinzi wake wakimsubiria.

“Nipekekeni chumba cha mawasiliano”

“Sawa mkuu”

“Na wewe ungana nasi”

Rahaba alimyooshe sekretari wake mkono, kwa haraka akaungana na raisi Rahab kuelekea katika chumba maalumu kilichopo chini ya Ardhi na huko kuna watu wanafanya kazi ya kuangalia kila kitu kinacho endelea duniani, hususani hapa Tanzania, ili kuhakikisha kwamba wanayawahi kuyazuia matukio yote ya kigaidi yanayo pangwa kufanywa. Wakaingia kwenye lifti iliyo washusha hadi chini, watu wote walipo muona Rahab, wakasimama kwa ajili ya kutoa heshima kwa raisi huyu.

“Kaeni endeleeni na kazi”

Rahab alizungumza huku akitembea hadi kwenye Tv kubwa inayo karibia kujaa ukuta mzima wa aneo hilo. Akatazama jinsi kazi za Satelait zinavyo endeshwa katika hili eneo, akajirdhisha kwa hilo.

“Wasilina ana wanziri mkuu wa Uingereza ili tuweze kuunganishwa moja kwa moja na wanajeshi wanao kwenda kwenye oparesheni hiyo”

“Sawa madam President”

Sekretari huyo alizungumza, akachukua mkonga wa simu maalumu inayo tumiwa katika ofisi ya raisi, akapiga simu katika ofisi ya waziri mkuu wa Uingereza, simu ikapokelewa na sekretari wa ofisi hiyo ya waziri mkuu, sekretari naye akamuunganisha waziri wake mkuu.

“Muheshimiwa waziri mkuu yupo hewani”

“Muweke loud speaker”

“Kila mmoja tunaomba akae kimya”

Sekretari alizungumza kwa sauti ya juu na kuwafanya wafanyakazi hawa zaidi ya mia moja na hamsini kukaa kimya. Sekretari akaminya kitufe cha simu hiyo na kuifanya sauti ya waziri mkuu wa Uingereza kusikika kwa kila mmoja.

“Muheshimiwa raisi, naada ya sekunde stini tunakuunganisha uweze kushuhudia oparesheni moja kwa moja”

“Nashukuru sana muheshimiwa waziri mkuu”

“Balozi wako naye ndio ameingia ofisini kwangu sasa hivi kuendelea kutazama ni kitu gani kitakacho endelea”

“Nashukuru pia kusikia hivyo. Ukihitaji msada wowote wa mimi kuweza kukusaidia usisite kuzungumza muheshimiwa waziri mkuu”

“Nashukuru kwa nafasi hiyo muheshimiwa raisi”

“Asante”

Raisi Rahab akakata simu, baada ya sekude kadha alizo kuwa anazugumza waziri mkuu, video maalumu kutoka kwa wanajeshi wapatao ishirini, walio valia kofia maalumu zenye kamera na vinasa sauti, ikaanza kuonekana, wakiwa ndani ya helicopter. Watu wote ndani ya hichi chumba wakabaki wameshangaa kwa maana hakuna hata mmoja anaye jua ni oparesheni gani inayo endelea. Rahab akaanza kiminya minya vidole vyake huku macho yakiwa yamemtoka.

“Madam President unaweza kukaa hapa”

Sekretari alizungumza baada ya kumtazama raisi Rahab anaye oneknaa kujawa na shauku kubwa sana ya kushuhudia oparesheni hiyo jinsi inavyo endeshwa na wanajeshi hao wa kimarekani.

“Tuna dakika moja kala ya kuingia kisiwani, jiandaeni kwa kuruka”

Ilisikika sauti kwenye Tv hiyo, watu ambao hawakuwahi kushuhudia oparesheni za kijeshi wakajiweka sawa kwenye viti vyao huku wakitamani kuona ni kitu gani kinacho endelea. Galfa watu wote ndani ya ukumbi huu wakastuka akiwemo Rahab, kwani helicopter moja ya wanajeshi hao imeshambuliwa na bomo na kulipuka yote. Wakiwa katika mshangao, helicopter ya pili nayo ikaanza kuyumba, baada ya kupunyuliwa na kombora lililo piga kwenye mabaka yake na kusababisha yakatike.

“Tunaanguka, ninarudia tena tunaanguk…….”

Hata kabla mwajeshi huyo hajamalizia sentensi yake Tv mzima ikajaa chenga cheka, yeusi na rangi ya kijivu ikimaanisha kwamba wanajeshi hao kwa sasa wamelipuliwa na bomo na kufa, hata kabla hawajaendesha oparesheni hiyo ya kumkomboa Sa Yoo na Junion Jr.


Taratibu raisi Rahab akanyanyuka kwenye kiti chake alicho kikalia huku akionekana kushangaa sana kwani haamini kwa kile anacho kiona. Watu wote ndani ya chumba hicho wakabaki kimya kwani jambo lililo tokea hakuna hata mmoja ambaye aliweza kulitarajia kuliona likitokea.

***

Mshangao huo si kwa nchi ya raisi wa Tanzania, ila hata viongozi waliomo katika ofisi za waziri mkuu wa Marekani wakabaki wakikaa kimya huku wengine wakisononeka kwa kile walicho kiona. Viongozi wa majeshi hususani wanao husika katika oparesheni hiyo wakazidi kushangaa kwa maana taarifa ya kwenda kuvamia katika kisiwa hicho ni wao pekee ndio wanao tambua, na wala hawakuwa na wazo la kumtilia maanani waziri mkuu wao kwani ni kiongozi anaye aminika na amebeba majukumu makubwa ya kitaifa.

“Muheshimiwa waziri mkuu vikosi vyetu vipo vime shambuliwa ni nini unahitaji tufanye?”

Mkuu wa jeshi la anga alizungumza huku akimtazama waziri mkuu.

“Hatuna haja ya kupeleke vikosi vyetu tena”

“Ila muheshimiwa waziri mkuu hatuwezi kurudi nyuma hii ni vita na hicho kisiwa kinaonyesha kimejaa magaidi wenye uwezo mkubwa sana kwa maana haiwezekani helicopter zetu na zenye wanajeshi wetu zishambuliwe kabla hata hazijatua ardhini”

Mkuu wa jeshi la anga alizungumza kwa msisitizo na kumfanya waziri mkuu kukaa kimya kwa muda ili kutafakari tukio hilo kwa mana akionekana kuleta upinzani katika hilo swala ana imani kwamba watu wanaweza kumshuku na kumuweke mashaka makubwa.

“Munahitaji tufanyeje?”

“Muheshimiwa waziri kuu hii ni oparesheni inayo husu inchi yetu sasa, hatuendi kwa ajili ya kuokoa mtoto na huyo binti, tunakwenda kushambulia maadui zetu, haiwezekani vijana wetu wakateketea na sisi tukaka kimya”

“Hata mimi ninaliunga mkono, ni laizma tushambulie kwa njia tatu ila kabla hatujaendelea katika hili pasipo kukuvujia heshima, muheshimiwa balozi wa Tanzania tunakuomba utupishe katika mipango hii”

Balozi wa Tanzania akamtazama waziri mkuu, ambaye kwa ishara ya machoa akamuomba aweze kutoka ndani ya chumba hichi.

“Muheshimiwa makamu wa raisi, kuanzia hivi sasa hatuhitaji mtu mwengine au nchi nyengine iweze kuhusika wala kutambua ni nini kinacho endelea. Mawasiliano na Tanzania ya hii oparesheni kuanzia sasa hivi tunayakata tutawapa maelezo tu ya nini kinacho endelea baada ya oparesheni kwisha”

Waziri mkuu akashusha pumzi baada ya kuona viongozi wake hao wa majeshi wamechachamma.

“Sawa”

“Na pasipo kukuvunjia heshimiwa, hauto ruhusiwa kuzungumza na simu hadi oparesheni iishe na kama una simu binafsi ninaiomba mkuu”

Mkuu wa jeshi la ardhi alisimama mbele ya waziri mkuu huku akimtazama usoni mwake. Waziri mkuu kidogo mapigo ya moyo yakamuenda kasi, ila akajikaza huku akimtazama mzee huyo, taratibu akaingiaza mkono wake kwenye mfuko wa koti alilo livaa na kutoa simu yake, akaizima kisha akamkabidhi mkuu huyo wa jeshi la ardhi.

“Ninaomba simu zenu wote”

Mkuu hiyo wa ardhi alizungumza huku akiwatazama watu wote waliomo kwenye hichi chumba, watu wakaanza kutoa simu zao na kumkabidhi mkuu huyo, simu zote zikaweka sehemu maalumu ambayo hakuna mtu ambaye anaweza hata kuiiba simu yake kiujanja kwa maana ni sehemu ambayo inaonekana na kila mmoja aliyopo ndani ya chumba hicho. Simu ambazo zimenaza kutumika ni simu maalumu za kujeshi ambazo zinawasiliana na wahusika katika fikosi husika ambavyo vimepewa kazi ya kuvamia kisiwa hicho kilichopo nje kidogo na nchi ya Uingereza. Mipango ilivyo kamilika kupangwa, amri ya utekelezaji ikatolewa na waziri mkuu, huku moyoni mwake, akimuomba msamaha John, kwani kisiwa hicho haju kitafanywa nini katika mashambulizi hayo ya kustukiza.

***

Sa Yoo hakuhitaji kusimama baada ya kuona kordo inayo elekea mbele, alicho kihitaji yeye ni kujikoa kutoka mikononi mwa maadui zake hao ambao anaamini kwamba wakimkamata ni lazima watamfanya kitu kibaya sana kutokana na kumuua mlizi aliye kuwa akimlinda. Swala la kuchoka hakuhitaji kuliruhusu kabisa akazidi kusonga mbele, milio ya risasi ambayo alianza kuisikia nyuma yake ndio ikazidi kumchanganya kabisa na kujikuya akizidisha kasi ya kukimbia, cha kumshukuru Mungu katika njia hiyo iliyopo chini ya ardhi kuna miwanyiko sita ya njia hizo zilizo eleke katika maeneo tofuto tofauti tofuati. Sa Yoo akakunja katika njia inayo elekea kushoto kwake, hakujali kama atakuna na kitu gani kayika njia hicho alicho kifanya yeye ni kuokoa maisha yake. Kila alivyo zidi kwenda ndivyo jisi magumaini mapya yalivyo jitokea, kwani aliweza kuona mwanga kwa mbali, akakimbia kama dakika kumi na kufanikiwa kufika katika eneo linalo ingiza mwanga kutokea juu, akakuta ngazi za chumba kama alizo zitumia kuingilia katika njia hiyo iliyopo chini ya Ardhi. Kwa haraka akaanza kupanda katika ngazi hiyo huku akitazama juu, akafika eneo la mfuniko huo ambao ni wa nondo, akausukuma kwa kutumia mkono wake wa kulia huku mkono wake wa kushoto ukiwa umeshikilia nondo ya ngazi aliyo panda. Juhudi ya nguvu yake yakaanza kuza kuzaa matunda, akafanikiwa kufungua mfuniko huo na kwa haraka akatoka juu, sehemu aliyo tokea ni kwenye msitu mdogo ambao upo pembezoni mwa habari. Kitu licho mshangaza ni mabaki ya kama helicopter yanayo endelea kuwaka moto.

‘Yesu wangu nini hichi?’

Sa Yoo alizungumza huku akitazama miliiya wa wanajeshi wawili inayo ungua kwa moto.

‘Sa Yoo fanya kitu, fanya kitu’

Sa Yoo alizungumza mwenyewe huku akiendelea kutazama huku na huku ili aweze kupata japo nafasi ya kutoroka katike eneo hili akiwa salama salmini. Kwa habati nzuri akaoona moja bunduki ikiwa imeanguka, kwa haraka akaiokota, akaikagua na kugundua ni nzima. Akiwa katika hatua za kuikagua akaona kusikia milio ya magari ikija katika eneo hilo, jambo lililo mfanya atafute kichaka kikubwa na kujificha. Gari ndogo za jeshi zipatazo sita zikafika katika eneo hilo, wanaume wote walio shuka katika magari hayo, Sa Yoo aliweza kuwatambua vizuri kwa maana ni wanajeshi wa John. Wanajeshi hawa wakaanza kuwakagua maiti za wanajeshi hawa wa Uingereza walio kufa. Wanajeshi hawa walivyo ona hakuna kiumbe chochote ambacho kipo hai katika eneo hilo wakaanza kushangilia huku wakipiga risasi zao angani wakionyesha wamejawa na furaha kubwa kwa tukio hilo. Ukimya wa gafla ukatawala, baada ya wanajeshi hao kumona Kimbery na vijana wake wakitoka katika shimo ambalo alitoka Jojo.

“Madam tumevamiwa, na jeshi la Uingereza ila tumefanikiwa kuwateketeza”

Mkuu wa kikosi hicho alizungumza huku akimtazama Kimbery usoni mwake. Kimbery akatazama mabaki ya helicopter hizo, hasira kali sana ikampanda.

“Kuna binti ametoroka, ninahitaji kuhakikisha kwamba munamsaka na apatikane haraka iwezekanavyo sawa”

“Sawa mkuu”

Kwa ishara Kimbery akamuru wanajeshi wote kutawanjika katika msitu huu na kuanza kumsaka Sa Yoo ambaye mwili mzima ukaanza kumtetemeka kwa woga kwani eneo lote hili limezingirwa na wala hafahamu ni wapi anaweza kutorokea.

***

Urafiki kati ya Adrus na Cookie ukazidi kupamba moto, kila mmoja akajawa na hisia kwa mawenzake, japo Adrus, anajaribu kujidanganya kwamba hawezi kumuingiza Cookie kwenye moyo wake ila tama ya kimapenzi kama mwanaume aliye rijali ikamjaa. Kila alipo mtazama Cookie usoni mwake na kujaribu kumshika mkono wake, basi jogoo wake aliweza kusimama akishiria kwamba anahitaji kitu kwa Cookie.

“Adrus”

“Mmmm”

“Ninaweza kukuamini?”

Cookie alizungumza kwa sauti ya upole sana huku akimtazama Adrus usoni mwake.

“Ahaa kwa nini unataka mimi nikumini?”

Cookie akaka kimya huku akimtazama Adrus usoni mwake, kwani swali hilo ni zito sana kwani kitu anacho kwenda kukizungumza ni kikubwa sana na wala hakutarajia kama anaweza kukizungumza kwa muda huu mfupi tangu amtambue Adrus.

“Adrus”

“Naam”

“Nina imani uliyo yazungumza hapo yote ni uongo, wewe sio mfanya biashara na wala huna duka unalo uza simu aina ya Iphone”

Maneno ya Cookie yakamstusha sana Adrus, hisia za mapenzi zote kikapotea moyoni mwake. Akamkazia macho Cookie, ila Cookie hakulijali hilo kwa maana tayari alisha jiandaa kisaikolojia kwani huu ni muda wa kupambana na Adrus katika swala zima la kihisia.

“Natambua wewe ni agent wa serikali, agent ambaye utakuwa ni msaada mkubwa sana kwa nchi ya Marekani”

“Shiiii…..wewe ni nani?”

Adrus alizungumza kwa sauti nzito huku akimtazama Cookie usoni mwake. Cookie akameza fumba la mate huku akimtazama Adrus usoni mwake, macho yoye ya kulegea yakamtoweka, kwa maana anafahamu kuanzia hivi sasa ni jambo lolote linaweza kujitokea.

“Mimi ni Cookie, msichana hatari ambaye nilipewa jukumu la kukuua wewe na watu ambao wanahitaji kusitisha mpango mzima wa wewe kuingia mikononi mwa jeshi la Marekani”

Cookie alizungumza kwa kujiamini, hapo ndipo Adrus akagundua ukali ambao Cookie anao kwani urembo wake wote umebadilika na kuwa ukatili ambao kwa mara ya kwanza hakuweza kuustukia kabisa.

***

Eddy taratibu akayafumbua macho yake, ukungu mwingi ulio mtawala machoni mwake ukamfanya ashindwe kuweza kuona vizuri vitu vilivyopo karibu yake. Mlio wa mashine inayo hesabu mapigo ya moyo wake ikamfanya aanze kuvuta kumbukumbu za kukumbuka ni wapi aliwahi kuusikia mlio huo. Ubongo wake wa kumbukumbu hakuweza kutoa jibu kwa haraka kwa maana bado hujarudi katika hali yake ya kawaida.

“Argraa”

Kelele ya Eddya ukawastua walinzi walipo nje ya chumba hicho kwa haraka walinzi wakaingia huku wakiongozana na Phidaya aliye mbeba Camila. Eddya kajaribu kunyanyuka kitandani ila walinzi wake wakamuwahi kumzuia.

“Kamuite dokta Jamani”

Phidaya alizungumza kwa haraka huku akimkabidhi Camila kwa moja ya mlinzi kwa maana yeye mwenye ni daktari ana anafahamu jinsi ya kumuwahi mgonjwa andapo anakuwa katika hali kama hiyo.

“Honey honey tulia”

“Junio yupo wapi?”

Eddy alizungumza kwa ukali huku akijitahidi kunyanyuka. Phidaya akabaki akiwa ameshikwa na butwaa, kwani mtoto ambaye mume wake anamuulizia tayari alisha kufa na walimzika na kusahau kabisa, kuhisiana na yeye.

“John pumbavu nikinyanyuka nitahakikisha ninakuteketeza mbweha wewe”

Eddy alizungumza kwa hasira, watu wote ndani ya chumba hichi wakagundua kwamba muheshimiwa anaanza kuchanganyikiwa. Dokta Benjamini kwa haraka akafika katika chumba alicho lazwa Eddy.

“Naombeni munipishe, samahani”

Dokta Ranjiti alizungumza kwa msisitizo huku akiwasogeza walinzi waliopo katika eneo hili. Walinzi wakatoka chumbani humu ila Phidaya akabaki akiwa amesimama pembeni ya kitanda hicho huku machozi yakimwagika usoni mwake, hakuhitaji kuamini kwamba mume wake anakwenda kuchanganyikiwa.

“Ehee Mungu wangu, mlinde mume wangu”

Phidaya alizungumza huku akiwa ameifumbata mikono yake kifuani mwake, hata wazo la mwanaye halikuwepo kwa wakati huu.

“John wewe kimbia tu na mwanangu, nitakuchinja, ninakuambia nitakuchinja”

Eddy aliendelea kuzungumza huku macho yakiwa yamemtoka, akionekana kabisa na mtu mwenye hasira. Dokta Benjamini kwa haraka akamchoma sindano ya usingizi Eddy na baada ya muda mfupi Eddy akalala fofo.

“Madam, muheshimiwa atakuwa salama”

Dokta Benjamini alizungumza kwa sauti ya upole huku akimmtazama Phidaya usoni mwake, taratibu Phidaya akaka pembeni ya kitanda alicho lazwa Eddy huku taratibu akianza kumshika mashavuni mwake. Mlinzi aliye pewa jukumu la kumshika mtoto akaingia chumbani humu ila kwa ishara ya macho dokta Benjamini akamkataza mlinzi huyo asimkabidhi Phidaya mtoto kwa sasa kwa maana akili yeka haipo sawa.

***

Shamsa kama mbogo aliye jeruhiwa kwa hasira, akamtandika Dokta Ranjiti ngumi ya pua, watu walio simama karibu yao wakabaki wakishangaa. Dokta Ranjiti kaha kabla hajaishika pua yake akastukia akipigwa kigoti cha sehemu za siri na kumfanya ajipinde huku akigugumia. Watu ambao sasa walikuwa wakijitahidi kuwaokoa watu aliomo ndani ya gari wakajikuta wakizunguka duara na kuwaweka Shamsa na Dokta Ranjiti kati ili waweze kushuhudia jinsi binti huyu wa kiarabu akitembeza kichapo kwa daktari huyu. Kam ilivyo kawaida, ya watanzania, mwenye simu yenye uwezo wa kuchukua video, huu sasa ndio ukawa wakati wake wa kuchukua tukio hilo la kustajabisha. Shamsa alivyo ona dokta Ranjiti amejikunja, akampiga kigoti cha kidevu na kumfanya mzee wa watu kuanguka mzima mzima, askari walio fika katika eneo hili kwa haraka wakajaribu kumshika Shamsa, ila mlinzi mwenye jukumu la kumlinda Shamsa katika eneo hili akachomoa bastola yake na kuwanyooshea askari hao wa usalama wa raisi, wasidhubutu kabisa kumshika Shamsa, jambo lililo mfamya Shamsa kumkalia dokta Ranjiti tumnoni na kuanza kumpiga ngumi mfululizo za usoni mwake na kuwafanya wananchi walio jisahau kama wapo eneo la ajali kuanza kushangilia kwa furaha sana huku wakimuhimiza Shamsa kuendelea kutoa adhabu ya makonde kwa dokta Ranjiti pasipo ya wao kufahamu ni kitu gani kinacho endelea katikati ya watu hao wawili.



“Niambie mwanangu yupo wapi?”

Shamsa alizungumza kwa msisitizo huku akimkaba koo dokta Ranjiti. Askari wakabaki kuwa mashuhuda wa tukio hili na ubaya wanashindwa kuelewa huyu binti ni mwana usalama kama jamaa aliye washikia bastola au ni binti wa kawaida.

“Si..juiui mimi”

Shamsa akamshindilia dokta Ranjiti ngumi ya pua na kumfanya pua yake kupinda kidogo na kuendelea kumwagikwa na damu.

“Hei nisaidie”

Shamsa alizungumza huku akimtazama mlinzi anaye mlinda, kwa haraka mlinzi huyu akamnyanyua dokta Ranjiti baada ya Shamsa kunyanyuka huku akihema kwa hasira na kuchoka.

“Naomba pingu”

Shamsa alimuambia askari mmoja huku akimnyooshea mkono wa kulia. Askari kwa haraka akamkabidhi Shamsa pingu, Shamsa akaishika mikono ya dokta Ranjiti, akairudisha kwa nyuma huku akisaidiwa na mlinzi wake, wakamfunga pingu na kuondoka naye katika eneo hili la ajali na kurudi naye eneo ambalo wamemuacha Phidaya na walinzi wengine. Wananchi wakabaki wakishangaa jinsi binti huyo alivyo hodari.

“Mamamaaeeeee, kuna mabinti sio wa mchezo mchezo, nyinyi fugeni mitako yenu mukishikiwa hata kiwembe munatetemeka hata kurusha ngumi hamuwezi”

Mpiga debe mmoja alizungumza huku akiwatazama wadada wawili walio jaliwa makalio makubwa ambao nao pia walikuwa ni miongoni mwa mashuhuda wa tukio hilo.

Walinzi wengine wakabaki wakishangaa kumuona Shamsa na mlinzi wakija na mtu ambaye anavuja damu usomzima.

“Vipi huyo?”

Mlinzi aliye mbeba Camila alizungumza huku akimtazama mlinzi mwenzake ambaye uso wake umejaa tabasamu sana kwani hakumfikiria Shamsa kama ni msichana ambaye anajiweza katika swala zima la kupigana.

“Mzee kala kipigo”

Mlinzi huyo alizungumza huku akicheka kidogo, akamkalisha dokta Ranjiti kwenye kiti kilichopo nje ya wodi hiyo. Shamsa akamtazama kwa muda dokta Ranjiti kisha akamtandika ngumi nyingine hadi walinzi wote wakastuka kwani hawakutekegemea ngumi hiyo nzito inaweza kupigwa na binti huyo mrembo ambaye baadhi yao walisha anza kumtamani ila ni siri ya mioyo yao, wanaogopa kupoteza nafasi ya kuilinda familia hii.

“Naamini jibu mumelipata”

Mlinzi huyo alizungumza huku akiwatazama wezake, Shamsa akaanza kumpapasa dokta Ranjiti kwa bahati nzuri akamkuta na simu mfukoni mwake. Akaichukua simu ya dokta Ranjiti, akaanza kuikagua, ila akashindwa kuifungua kutokana na namba za siri.

“Nitajie namba za siri”

Shamsa alizungumza kwa ukali huku akimkazia macho dokta Ranjiti.

“Ha..hahaa…”

Dokta Ranjiti alicheka kwa dharau, akamtemea Shamsa fumba la mate lililo jaa damu. Shamsaakafumba macho yake kwa muda huku kifua chake kikipanda na kushuka kwa kasi sana, walinzi wote wakakaa kwenye usikivu wa kusikilizia ni kitu gani ambacho mzee hoyo atafanywa kwa kitendo chake cha dharau alicho kifanya.

***

“Adrus sihitaji kukudhuru, sihitaji kukufanyia kitu chochote kibaya kwa maana nimeona huna hatia yoyote ya mimi kuweza kufanya ubaya dhidi yako, ninacho kuomba ukubaliane na mimi kwa kile ninacho kwenda kukizungumza”

Cookie aliendelea kuzungumza kwa msisitizo huku akimtazama Adrus usoni mwake.

“Wamarekani watakausabisha maisha ambayo sihitaji kabisa yaweze kukutekea. Macho ya makundi mengi ya kigaidi kwa sasa yanakutazama wewe, kuna maelfu ya watu wanakutazama wewe pasipo wewe mwenyewe kuweza kufahamu. Si wewe tu ila hata mama yako wapo watu ambao wanamtafuta, pesa alizo kabidhiwa na wamarekani, hazito weza kumsaidia, kwa maana kosa lako moja litasababisha kufa kwa mama yako”

Maneno ya Cookie yakazidi kumshangaza Adrus, wasiwasi mwingi ukamjaa sana.

“Vikundi vya magaidi, hujitoa muhanga kuhakikisha kwamba wanamuua Naomi, msichana ambaye ulishirikiana naye kwenye oparesheni nchini Pakistani, kosa lenu linao lasabishwa nyinyi kuwindwa kwa kipindi chote ni kitendo cha kumua mjomba wa kiongozi wa kikundi cha Al-Quida, nina imani unaweza kuona ni jinsi gani balozi kadhaa za Marekani zilivyo kuwa zikishambuliwa kipindi mupo nchini Pakistani, chanzo mulikuwa ni nyinyi.”

Maneno yote aliyo yazungumza Cookie, Adrus anayafahamu kwani ndio ukweli wa maisha aliyo yapitia, kabla hajarudi nchini Tanzania.

“Adrus, sikuwahi kumpenda mwaume yoyote kwenye maisha yangu, na wala sikuwahi kufikiria kupenda mwanaume, kazi yangu ni kuua tu, ila kwako nimejisikia mkosefu, sihitaji kukua, sihitaji damu yako iwe mikononi mwangu. Umeniteka moyo wangu kwa muda mfupi na wala sihitaji kujitia maamuzi yangu ya kufichua siri yangu kuwa na wewe ninahitaji tukimbie mbali na mikono ya hawa magaidi tukatafute maisha mimi na wewe tuweze kuishi kwa amani na upendo, tujenge familia yetu. Nakuomba msahau Naomi, ninakuomba Naomi usijaribu hata kumfikiria kwani unaweza kuhatarisha maisha ya mama yako pamoja na raisi wako. Tafadhali ninakuomba Adrus nipo chini ya miguu yako”

Cookie alizungumza kwa sauti ya chini sana ambayo hakuna mtu yoyote ambaye anaweza kusikia, zaidi ya Adrus peke yake. Kigugumizi kikautawala mdomo wa Adrus, ulimi ukashindwa hata kunyanyuka na kuunda japo neno Taarifa alizo zisikia ni kubwa mmno ambazo kusema kweli kwa mtu mwenye mapenzi na mama yake ni lazima afanye maamuzi magumu tu.

“Kubali kupoteza kazi, kubali kupoteza kila kitu, nina kuhakikishia kukulinda na kukuepusha na kila adui ambaye atakusogelea”

“Cookie”

“Bee”

“Nitakumini vipi kama hayo unayo zungumza ni kweli?”

Cookie akatoa simu yake mfukoni mwa suruali aliyo ivaa. Kwa haraka akamtafuta mama yake Adrus kwa kupitia satelait, alipo hakikisha kwamba amempata akamuonyesha Adrus.

“Nina imani huyu ni mama yako”

Adrus akastuka sana baada ya kumuona mama yake akizungumza na mwanaume mmoja katika eneo lililo jaa magari mengi sana ya kununua.

“Huyu ni mama yako, soon atakuwa mama yangu mkwe, ikiwa nimeweza kumtafuta mimi kwa muda mchache sana na kuweza kumpata, je timu ya watu walipo nyuma yangu je watafanyaje. Lifikirie hili Adrus, ukiingia mikononi mwa serikali ya Marekani, mama yako na nchi yako unaiweka kwenye list ya mashambulizi ya kigaidi, ukiingia mikoni mwa magaidi, kichwa chako kitakuwa ni malipo ya kifo cha mjomba wa kiongozi wa Al-Quida. Kuungana na mimi, itakuwa ni njia sahihi ya sisi kuweza kutatua matatizo yote taliyopo mbele yetu. Sasa chagua, moja kati ya mamabo hayo matatu niliyo kueleza.”

Cookie aliuzungumza kwa msisitizo na kumfany Adrus kushusha pumzi nyingi huku akimtazama Cookie usoni mwake akishindwa hata achague lipi kwa muda huo

***

Wanajeshi walio amrishwa na Kimbery kumsaka, wakazidisha umakini katika kumtafua msichana waliye ambiwa. Sa Yoo hakujali bunduki aliyo kuwa nayo, kitu kinacho weza kumsaidia kwa sasa ni kumuomba Mungu wake tu afanye japo muujiza aweze kufanikiwa kuto kuingia mikononi mwa wanajeshi hawa. Mwili mzima ukaanza kumtetemeka, kila mwanajeshi anaye pita karibu na kichaka hicho alicho jificha anahisi kufa kufa.

‘Ehee Mungu wangu nisaidie mimi’

Sa Yoo alizungumza huku akiwa amejikunyata, bunduki alio kuwa amiokota ikamshinda uzito wa hata kuiendela kuishikilia, na kujikuta akiingusha chini.Kishindo cha bunduki hiyo kuanguka chini kikamstua mwanajeshi mmoja ambaye yupi hatua chache kutoka katika kichaka hicho. Mwanajeshi huyo akaanza kunyata kwa umakini sana huku bunduki yake akiwa ameishika mkononi. Hatua za mwanajeshi huyo kukinyemeleaa kichaka hicho zikamfanya Sa Yoo kugeuka nyuma na kumuona mwanjeshi huyo akiwa amebakisha mita chake kabla hajayafunua majani mengi yaliyo kifunika kichaka hicho. Gafla mwanajeshi huyo akaanguka chini mzima mzima, jambo lililo mstua sana Sa Yoo. Milio ya risasi ikaanza kurindima katika eneo hili. Sa Yoo atazama eneo la baharini na kuona meli kadhaa za wanajeshi zikiwa zimesimama katika eneo hilo huku wanajeshi wengi wanao onekana ni wa jeshi la Uingereza wakizi kushambulia kisiwa hicho. Wanajeshi walio kuwa akimtafuta Sa Yoo, zoezi sasa likabadilika na kuamia katika kujaribu kuwazui wanajeshi hao wa serikali waisiingie katika ngome yao. Ila kwa jinsi jeshi la serikali lilivyo kipanga, wanajeshi hao wanao ongozwa na Kimbery wakajikuta wakishindwa kabisa kuhimili mashambulizi hayo ya wanajeshi wa serikali na wengi wakajikuta wakiangamia. Machozi ya furaha yakaanza kumminika Sa Yoo, kwani anaamini muda wa kuwa katika mikono salama sasa umewadia.

Ndege sita za kijeshi zilizo jaa mabomu huku zikiongozwa na marubani wenye uwezo wa hali ya juu ya kukabiliana na mashambulizi ya aina yoyote katika uwanja wa vita, zikaanza kufanya kazi yao. Kama amri ya wakuu wao wa jeshi ni kugakikisha kwamba wanaiteketeza ngome ya maadui hao pasipo huruma ya aina yoyote.

Ndege hizo zikashambulia ndege za jeshi la John ambazo ndio kwanza marubani wake walikuwa wakijiandaa kuzipaisha angani ili kukabiliana na mashambulizi hayo ya anga.

Sa Yoo hakujali hatari ya kupigwa risasi, alicho kifanya ni kutoka kasi katika kichaka alicho jificha huku mikono yake akiwa ameionyoosha hewani ili hata wanajeshi wa serikali wasimjumuisha na magaidi hao. Sa Yoo akazidi kutimua mbio kuelekea katika fukwe walipo wanajeshi hao.

Kimbery akayang’ata meno yake kwa hasira baada ya kumuona Sa Yoo akikimbilia katika fukwe hizo.

“Tuondokeni, tutamtafuta tu”

Kimbery aliwaambia vijana wake wawili walio jibanza kwenye moja ya mti mkubwa, wakiendelea kutazama jinsi wanajeshi wao wanavyo teketea. Wanajeshi wa Uingereza wakamtambua Sa Yoo, kwani walisha onyeshwa picha zake wakiwa wanjianda kuingia katika oparesheni hii. Kwa haraka wanajeshi wawili wakamimbilia Sa Yoo, huku wengine wakiendelea kuwalinda kwa kuwashambulia wanajeshi hawa wanao malizikia malizikia. Wakakimbia na Sa Yoo hadi kwenye moja ya boti na kumpakiza.

“Mtoto yupo wapi?”

Mwanajeshi mmoja alizungumza huku akimtazama Sa Yoo usoni mwake.

“Sifahamu ila aliiondoka na mkuu wao”

“Mkuu wao ni nani?”

“John”

“Waheshimiwa tumempata makeka mmoja bado mtoto”

Mwanajeshi hiyo alizungumza kwa simu ya upoepo aliyo ishika mkononi mwake.

‘Endeleni kumtafuta, huyo binti arudishwe makao makuu’

“Sawa mkuu”

Mwanajeshi huyu akawaamuru wezake wawili kuodoka na Sa Yoo kwa boti ya mwendo wa kasi katika hilo eneo kisha wao wakazidi kusonga mbele kuhakikisha kwamba wanamukoa Junion Jr pasipo kujua kwamba mtoto huyo alisha ondoka katika eneo hilo muda mrefu sana ulio pita.

***

Shamsa akayafumbua macho yake yaliyo jaa uwekundu ulio tokana na hasira kali, akajifuta mate aliyote temewa usoni mwake. Akapiga hatua nyima mbili nyuma, akamtazama dokta Ranjiti jinsi alivyo kaa katika kiti hicho, kwa kasi ya ajabu Shamsa akampiga dokta Ranjti teke la shingo hadi akaanguka yeye na kiti chake. Kishindo cha kuanguka kwa dokta Ranjiti kikamstua Phidaya aliyopo ndani ya chumba alicho lazwa Eddy, kwa haraka akatoka na kushangaa kumkuta dokta Ranjiti akinyanyuliwa na Shamsa.

“Ranjitiii”

Phidaya aliita kwa ukali huku akimtazaama ranjiti aliye kalishwa kitako na Shamsa.

“Nitajie namba za siri”

“Sitaji”

Dokta Ranjiti alisimamia msimamo wake, wa kuto kutaja namba ya siri, kwani simu yake hiyo imekusanya nyaraka zinazo weza kumuonyesha John sehemu alipo. Shama akamtazama mlinzi mmoja kwa jicho la kuiba, akaiona bastola ya mlinzi huyo aliyo ichomeka kiunoni mwake.

“Sawa kama huitaji kunipa namba zako za siri”

Shamsa alizungumza kwa sauti ya upole huku akimsogelea mlinzi huyo ambaye wala hatambui ni kitu gani ambacho Shamsa amepanga kukifanya. Kwa haraka Shamsa akaichomoa bastola ya mlinzi huyo aliye baki akiweweseka, asijue hata ni kasi ya aina gani Shamsa ameitumia katika kuichukua bastola yake. Shamsa akamuelekezea dokta Ranjiti bastola hiyo, jambo lililo mfanya Phidaya macho mkumtoka kwa mshangao.

“Sina huruma, ninahitaji unitajie namba za siri la sivyo nina kufumua ubongo wako”

“Shamsa ni nini unacho taka kufanya”

“Mama tulia hili halikuhusu”

“Linamuhusu”

Dokta Ranjiti alizungumza huku akitabasamu, kwa hasira ambayo Shamsa, imempanda, mwili mzima ukaanza kumtetemeka, akatamani japo kufyatua risasi amalize dokta Ranjiti ila akashindwa kabisa kwani huyo ndio ufunguo wa pekee ambao unaweza kumsaidia kumpata mwaye Junion. Jr.

“Mke wangu Phidaya nimekusimiss sana”

Walinzi wote wakazidi kushangaa kusikia mzee huyu anasema mke wa makamu wa raisi ni mke wake.

“Pumbavu funga bakuli lako, mimi si mke wako”

Phidaya naye akawa mkali.

“Hahaa, nimetoka huko nilipo toka nimekuja kwa ajili yako mke wangu, Phidaya, ninakupenda. Wewe ndio mwanaume uliye teke hisia zangu za maisha yangu”

Phidaya kwa hasira akajikuta akichukua jukumu la kumpokonya Shamsa bastola na kuichukua yeye, akaikoki na kumuelekezea dokta Ranjiti ambaye akaendelea kutabasamu.

“Ukiendelea kuzungumza ujinga wa aina yoyote nitakumwaga ubongo wako, sihitaji ujinga na familia yangu, mume wangu na mwanangu sawa”

“Hahaaa……Phidaya niue. Ukiniua wewe nitajisikia amani, ila kabla sijakufanya unatakiwa kufahamu ukweli kati ya huyo unaye muita mwanao Shamsa na mume wako anaye pigania maisha huko ndani kwani yeye na mimi sote ni wafu watarajiwa”

Maneno ya dokta Ranjiti yakamfanya Shamsa ahisi miguu ikinyong’onyea kwani katika maisha yake yote amejitahidi kuificha siri ya yeye kuwa amezaa na Eddy ambaye anamuheshimu kama baba yake. Phidaya akamtaza Shamsa, kisha akamtazama dokta Ranjiti.

“Zungumza hiyo siri”

Phidaya alizungumza kwa sauti iliyo jaa msisitizo na kumfanya dokta Ranjiti kumtazama Shamsa, kisha akatabasamu kwa muda na kukaa vizuri ili afunguke ukweli wa mambo yanayo endelea kati ya Shamsa na Eddy.



“Shamsa na huyo mume wako, wamezaa mtoto”

Dokta Ranjitii alizungumza kwa msisitizo na kumfanya Phidaya kucheka, kwa maana anao kilicho zungumwa ni uongo na ujinga tu.

“So ni hilo?”

Swali la Phidaya likamshangaza hata Shamsa mwenyewe ambaye mapigo yake ya moyo yanamuenda mbio.

“Ukihitaji kudhibitisha hilo chukua simu yangu”

Dokta Ranjiti alizungumza huku akimtazama Phidaya usoni mwake. Phidaya akamgeukia Shamsa, akaitazama simu aliyo ishika Shamsa.

“Chukua simu, hiyo ndio ina ukweli wa kila kitu ya uchafu ambao ameufunya mume wako na huyo unaye hisi ni mwanao. Hawakupendi hao ni watu wabaya kwako, mimi ndio mume wako sahihi”

“RANJITI NYAMAZAAAAAAAAAAAAAAAA”

Phidaya alizungumza kwa hasira huku mwili mzima ukimtetemeka.

“Shamsa naomba simu”

Shamsa mwili mzima ukamtetemeka, kwa haraka Phidaya akampora Shamsa simu aliyo ishika, kwa haraka Phidaya akaikagua namba ya simu.

“Nitajie namba yako ya siri”

“Phidaya”

“What?”

“Ni Phidaya, anza na P kubwa na herufi zinazo fwatia ziwe ndogo”

Phidaya akashusha pumzi huku akiandika herufi za jina lake. Kwa bahati nzuri simu ikafunguka.

“Ehhee ingia kwenye eneo la video”

Shamsa mwili ukazidi kumtetemeka, walinzi wote wakakaa kimya huku wakimtazama Phidaya anaye ipekua simu hiyo. Phidaya hakuona video ya aina yoyote.

“Ipo wapi hiyo video?”

Maneno ya Phidaya yakamfanya Shamsa kuitazama simu hiyo kwa kuiba iba, macho yakamtoka dokta Ranjiti, akaitazama simu yake. Kwani hajui ni kitu gani ambacho kimetokea hadi video hizo kuto kuwepo kwenye simu yake.

“Mwanaume mzima huoni aibu umeamua kuja kunigombanisha na familia yangu, eheee. Sasa ninakuambia nitakuua kwa mkono wangu mimi mwenyewe”

“Mama”

Shamsa aliita kwa sauti ya chini huku akimtazama Phidaya usoni mwake.

“Tusimuue sasa hivi, tumuache adhabu hiyo aje kukabidhiwa na baba”

Shamsa akaufikiria ushauri alio pewa na Phidaya, taratibu akatabasamu huku akimtazama Shamsa, akamkabidhi Shamsa bastola hiyo na kumchukua mwanaye.

“Eddy akiamka, ataikata shingo yako”

Phidaya alizungumza huku akitabasamu. Shamsa akaichukua simu ya dokta Ranjiti huku akitabasamu, akaiingiza mfukoni mwake, huku kirohoni akichekelea sana kwa jinsi alivyo iiba memory card ya simu hiyo hakuna mtu aliye weza kumuona wala kugundua.

“Utakufa, ninaomba tuondoke naye hapa hospitalini”

Shamsa alizungumza huku akizungumza na mlinzi aliye kuwa naye kwenye tukio la kumkamata dokta Ranjiti. Wakatoka nje na kuingia naye ndani ya gari.

“Tunampeleka wapi?”

“Kwenye nyumba ya zamani tulio kuwa tunaishi”

“Sawa madam”

***

Macho ya hasira yakaanza kumlenga lenga John usoni mwake, kwa kupitia mitambo ya satelait, akashuhudia jinsi wanajeshi katika kisiwa chake wakiteketezwa, majumba na hazina kubwa aliyopo katika kisiwa hicho yote yanateketezwa. Kwa hasira akaizima tv iliyomo ndani ya chumba chake, kisha akamtazama mtoto wa Eddy, kwa haraka akachomoa bastola yake na kumnyooshea mtoto huyo ambaye bado ni mchanga na haelewi ni nini kinacho endelea. Tabasamu la Junion Jr, likamaliza John nguvu kabisa, roho ya haya na kujihukumu ikaanza kumuingia moyoni mwake, kwani hakuna sababu ya msingo ambayo yeye anaweza kumuua mtoto huyo ambaye hastahili adhabu hiyo.

‘Wewe ndio utakuwa adui wa baba yako na wewe ndio utamuua baba yako’

John alizungumza kimoyo moyo huku akiungana na Junion Jr katika kutabasamu. Akanyanyua Junion aliye kuwa amemlaza juu ya meza na akamuweka begani mwake na kuanza kumbembeleza. Mlango wa chumba chake ukagongwa akamruhusu mtu anaye gonga. Mlango ukafunguliwa na akaingia mllinzi wake.

“Muheshimiwa mtu aliye nyuma ya mashambulizi hayo yote ni raisi wa Tanzania Bi Rahab”

“Nalitambua hilo”

“Unahitaji nini tufanye dhidi yake?”

John akaka kimya huku akitafakari ni kitu gani azungumze, akamtazama mlinzi wake.

“Nitawaambia nini tufanye, ni lazima alipe kwa hili tukio lililo jitokeza.

John alizungumza kwa msisitizo huku kwenye mawazo yake akiiona sura ya Rahab anaye onekana kufurahishwa kwa oparesheni nzima iliyo endeshwa.

***

Simu ya mkononi mwa Rahab ikaanza kuita, kwa haraka akitoa mfukoni mwake na kukuta ni namba ya waziri mkuu wa Uingereza, kwa haraka akaopokea, na kuiweka simu sikioni mwake.

“Habari za muda muheshimiwa raisi”

“Salama nipe riponi muheshimiwa waziri mkuu ni kitu gani kinacho endelea?”

“Oparesheni imekwenda vizuri, Sa Yoo amaokolewa ila hadi sasa wanajeshi wetu wanaendelea kumtafuta mkuu wa kikosi hicho alicho anaye itwa John anasadikika yeye bado anamshikilia mtoto mdogo wa muheshimiwa.”

“JOHN?”

Rahab aliuliza kwa msisitizo.

“Ndio, vipi unamfahamu?”

Rahaba akaka kimya huku akitafakari jibu la kumjibu waziri mkuu wa Uingereza.

“Hapana, ila ninashukuru kwa ushirikiano wenu na niweze kutoa pole kwa kupoteza wanajeshi katika oparesheni hii”

“Usijali ni moja ya changamoto za oparesheni za kijasusi, ila tunashukuru Mungu tumeweza kujua ngome kubwa ya kigaidi ambayo ilikuwa katika kisiwa hicho”

“Sawa, ila kama inawezeakana nitaomba bintu hiyo aweze kupata msaada wa kuletwa nchini Tanzania”

“Usijali katika hilo muheshimiwa raisi, nitafanya hivyo”

“Nashukuru sana waziri mkuu”

Rahab akakata simu yake, kisha akafunguliwa mlango na mlinzi wake na kuingia ofisini kwake. Akatembea kwa haraka hadi kilipo kiti chake, akataka kukaa, akakitazama kwa muda akashusha pumzi nyingi na kugairi kuendelea kukaa ofisini humo. Akaitoa simu yake mfukoni, akaitafuta namba ya Shamsa, akaitazama kwa sekunde kadhaa, kisha akaminya kioo cha simu katika alama inayo ruhusu kumpigia mtu simu. Simu ya Shamsa ikaanza kuita, kisha ikapokelewa.

“Za muda Shamsa”

“Salama ni kitu gani kinacho endelea?”

“Sa Yoo amepatikana”

“Ohoo asante Mungu, mwanangu je?”

“Wanajeshi wa nchi Uingereza bado wanaendelea kumtafuta John inavyo sadikika yeye ndjio ameondoka na Junion”

Ukimya ukatawala, Rahab akatambua moja kwa moja ni lazima Shamsa atakuwa amejawa na huzuni kubwa sana.

“Shamsa?”

Raisi Rahab aliita kwa sauti ya upole, akasikia sauti ya kiume ikicheka ambayo kidogo ikmastua. Akasikia mguno wa maumivu.

“Nitakuua kaa kimya”

Sauti ya Shamsa akizungumza kwa ukali ikasikika upande wa pili wa simu.

“Shamsa kuna nini kinacho endelea?”

“Hadi hapa nimemkamata dokta Ranjiti nina imani kwamba yeye ndio atakuwa kiongozi atakeye tuongoza katika oparesheni ya kumtafuta mwanangu”

“Ranjiti yupo nchini hapa?”

“Ndio, ninakuomba uweze kunisaidia katika ulinzi hivi sasa tunatoka Muhimbili tunaelekea katika nyumba tuliyo kuwa tunaishi”

“Okay, ninahiji kumuona huyo mshenzi, nitawakuta katika eneo hilo sawa”

“Sawa”

Rahab akakata simu na kutoka ofisini kwake. Akamuamuru mlinzi wake kutoa taarifa ya msafara wake, hawa wanatoka gari zilizo jaa walinzi wake, zimesimama aneo maalumu na wote wanaonekana wakimsubiria raisi.

Rahab na mlinzi wake wakaingia katika gari analo litumia na kuondoka katika eneo hilo.

***

“Nipo tayari kuungana na wewe, ila ninakuomba unihakikishie ulinzi wa mama yangu kwa maana ndio mtu pekee aliye baki katika familia yangu”

Adrus alizungumza huku akimtazama Cookie usoni mwake.

“Usijali, mama yako nitahakisha ninamugiza mtu na kumleta kule tutakapo kuwa tumekimbilia”

“Ila kwa nini Cookie umeamua kuwasaliti watu wako?”

“Ni kwa sababu ninakupenda Adrus, na wala haustahili kifo”

Adrus akamtazama Cookie kwa muda, moyo wake ukajikuta ukianza kumuamini sana Cookie.

“Sasa hii ndege inakwenda kutua nchini Marekani hapo itakuwaje?”

“Hapana ni lazima itatua nchi mbili kabla ya kufika nchini Marekani, kwenye nchi ya kwanza nina imani ndiopo tutakapo shuka na kutomea ambapo Mungu atatusaidia, kikubwa ni kuhakikisha kwamba tunawakimbia maadui wetu wasiweze hata kutukamata”

“Ila mama yangu amepewa pesa na nchi ya Marekani je wakizizuia?”

“Tutazihamisha katika akaunti ambayo haijulikani na baada ya hapo tutajua ni nini kinacho fwata”

“Sawa”

***

Taratibu mlinzi anaye mlinda Shamsa, akasimamisha gari nje ya geti kubwa la jumba la Eddy, Shamsa akashuka na kuzungumza na wanajeshi wanao linda hapa getini.

“Ila hatukufahamu na nyumba hii kwa sasa ipo chini ya uangalizi wa jeshi”

“Ninalitambu hili, ila mimi ni mtoto wa makamu wa raisi, nina kuna kazi maalumu ninahitaji kuifanya ndani ya nyumba ya baba yangu”

“Samahani madam hatuwezi kukuruhusu kuingia humu ndani kwa maana huna kitambulisho cha aina yoyote na hatuwezi kukuamini kwa maneno”

Shamsa akamawatazama wanajeshi hawa walio muwekea mkazo mkubwa sana.

“Nimekuja na mlinzi wa raisi Rahab, naye ana vitambulisho, ninaomba muniruhusu kuingia humu ndani”

“Muambie atupatie kitambulisho chake”

Shamsa akalitazama gari alilopo mlinzi huyo pamoja na dokta Ranjili aliye mpiga na kitako cha bastola alipo kuwa akizungumza na raisi Rahab na kumpelekea kupoteza fahamu. Kwa ishara Shamsa akamuita mlinzi hiyo, taratibu akashuka kwenye gari, na kuwasogelea Shamsa na wanajeshi hawa sehemu walipo simama.

“Wanahitaji kitambulisho chako”

Mlinzi huyo akatoa kitambulisho chake na kumkabidhi mwanajeshi mmoja akakisoma huku akimtazama mlinzi huyu.

“Ni kitu gani ambacho kinawaleta hapa ndani?”

“Kaka nimechoka kwa maswali ya kipuuzi, au unaona raha kuendelea kutusimamisha hapa nje tena mbele ya nyumba ya baba yangu eheee?”

Shamsa alizungumza kwa ukali hada wanajeshi hao wakastuka.

“Fungueni geti nipite kwa manaa hata raisi mwenyewe yupo njiani kufika katika eneo hilo”

Wanajeshi hawa wakatazamana.

“Samahani tunafwata amri tuliyo pewa kwamba hakuna mtu yoyote kuingia humu ndani, tunakuomba muingie katika gari lenu na kuondoka katika eneo hilo haraka iwezekanavyo”

Shamsa kwa haraka akichomoa bastola aliyo kuwa ameichomeka kiunoni mwake, eneo la nyuma. Akawanyooshea wanajeshi hawa ambao nao wakamnyooshea bunduki zao.

“Ukifyatua risasi, na sisi tunafyatua. Tunaifanya kazi yetu na si kuisikiliza kelele zako”

Mlinzi wa Shamsa akajikuta akikaa kimya huku akikosa kitu cha kufanya. Dokta Ranjiti taratibu akayafumbua macho yake, akatazama pembeni ila hakumuona Shamsa, akatazama siti ya mbele hakumuona mlinzi ambaye alikuwa anaendesha gari hilo. Taratibu akanyanyua kichwa chake, hakuamini macho yake alipo waona wanajeshi pamojana Rahab wakiwa wametunishiana misuli huku mlinzi akiwa amesimama kama bendera tu. Dokta Ranjiti taratibu akatabasamu, akafungua mlango wa upande wa pili wa gari hilo taratibu, akatoka ndani ya gari na kuurudishi malango huo.

‘Shamsa utalipa kwa hili, umenikosa’

Dokta Ranjiti alizungumza huku akitazama ni barabara ipi anaweza kutorokea, katika eneo hili lililo tulia na lina majumba mengi ya kifahari yanayo milikiwa na watu wenye pesa zao hapa nchini Tanzania.

 ITAENDELEA

1 comment:

BLOG