Search This Blog

Wednesday, November 18, 2020

MY LIFE SEHEMU YA 5/10

 

 


 MY LIFE

WRITER…………………………………………EDDAZARIA G.MSULWA
WEBSITE………………………………………… www.storyzaeddytz.com
CONTACT……………………………………….. 0657072588/0768516188
AGE……………..18+

SEHEMU YA 5 KATI YA 10

 



“Samahani”

Nilizungumza kisha nikatoka nje huku nikiwa nimeishika simu yangu mkononi. Nikafunga mlango huu wa ofisi kisha nikaipokea simu yangu.

“Haloo”

Niliita kwa sauti ya chini ila mtu aliye nipigia simu hakuzungumza kitu cha aina yoyote zaidi ya kukaa kimya. Nikarudia kuita zaidi ya mara nne ila mtu huyo hakuniitikia, nikaitazama namba hii kisha nikakata simu na kurudi tena ndani ya ukumbi. Nikaka kwenye kiti changu, Clara akanisogelea kidogo.

“Trela ya filamu ya Love Mask, ipo tayari kwenye tv tunaweza kuitazama?”

“Yaa”

Dokta Clara akaruhusu mfanyakazi anaye shuhulika na maswala ya editing ya filamu za kampuni yetu kuwasha tv. Trela hii ikaanza kuonekana kwenye Tv kubwa ya inch 60. Msisimko mkubwa ukaanza kunitawala mwilini mwangu, kwani ni trela ambayo kusema kweli ina msisimko mkubwa sana na ina matukio makubwa, ambayo katika kipindi cha kuirekodi hii filamu nilichukulia ni kawaida sana. Milipuko ya ajali za magari pamoja na majibizano ya risasi, yametawala sana kwenye hii trela. Kwa haraka haraka mtu anaweza kuhisi filamu hii imetengenezwa Hollywood. Hadi trela hii inaisha tukajikuta tukipiga makofi kwa shangwe, kwani ni kitu ambacho hatukutarajia kukiona kwa ukubwa kama huu.

“Jamani hembu irudieni tena”

Nilizungumza huku nikimtazama kijana huyu tunaye muita Tude Clasi.

“Hivi hii ndio mara ya kwanza watu kuiona hii trela ehee?”

Nilimuuliza dokta Clara kwa kumnong’oneza.

“Ndio, Tude alikuwa haitaji tuweze kuoona kabisa, yaani kazi aliifanya yeye na wale wachina walio ondoka"

“Ahaaa, sasa mulipangaje juu ya kuzindua hii trela?”

“Mama aliatuambia mwenye maamuzi ni wewe kwa sasa”

“Ahaa….., na mimi nasikilizia mipango yenu mumejiandaaje?”

Dokta Clara akasimama, akawaomba wasichana wawili kufunga mapazia ya ndani humu kisha taa zikazimwa na na giza likatawala kidogo. Ikawashwa Projecta iliyo angaza katika moja ya ukuta ambao ni mweupe. Akachukua maiki ndogo na kuivaa vizuri sikiuoni mwake. Akasimama sehemu ya ukuta huo.

“Hariri zenu?”

“Sauti yake ikasikika kwenye vipaza sauti vilivyomo humu ndani.

“Salama”

“Nilikuwa ninajadiliana na mkuu pale mambo mawili matatu. Kwa wale ambao hawamfahamu mkurugenzi mtendaji na mmikiki wa kampuni yetu ni yule pale Bi Jojo Eddazaria. Kampuni yetu ilianza na wafanyakazi thelathini kipindi ilipo kuwa inanaaza, ila hadi sasa hivi tumefanikiwa kuongeza wafanyakazi wapatano arobaini na tano na kufika idadi ya wafanyakazi sabini na tano.”

Dokta Clara alizungumza huku picha za wafanyakazi wa kampuni nzima wakionekana.

“Kampuni kwa kupitia meneja wake mpya ambaye ni mimi Clara Msanja. Kwa kushirikiana na wafanyakazi tumeweza kukuza mifumo ya social media, zetu ikiwemo akaunti ya Faceebok, Twitter, Instergram na Youtube Chanel yetu. Hapo awali tulikuwa na mafashabiki laki moja kwa Facebook ila kwa sasa tuna mashabiki milioni mia tisa, tisini na tisa elfu na mia nane. Tumebakisha idadi ndogo snaa kufika watu bilioni moja. Tukija kwa Instergaram hivi sasa tuna watu bilioni mbili, duniani kote, Twitter tuna watu milioni mia tano, na Youtube Chanel tuna mashabiki walio jiunga na chanel yetu duniani kote Bilioni ishirini na tano.”

Nikapiga makofi taratibu, kwani kwa kiwango tulicho kifikia kwa kweli tunaweza kutengeneza pesa nyingi sana.

“Kwa dunia ya sasa hivi tumeona kwamba mitandao ya kijamii ina nguvu kubwa sana kuliko hapo awali. Hatukuishia hapo tu, kuna watu hadi leo bado hawana Facebook, Instergram, Whatsapp, au Twitter au Youtube. Watu hao tumeamua kuhakikisha kwamba tunasambaza mawakala ambao watakuwa wanauza filamu zetu kwa CD original. CD zetu zitakuwa na ubora ambao kwa Tanzania haujawhi kutokea, ubora wake ni kwamba kwa mtu ambaye atajaribu ku-copy kwenye laptop au computer basi huo ndio utakuwa ni mwisho wa kifaa chake hicho”

Nikanyoosha mkono wangu wa kulia juu kidogo.

“Ndio mkurugenzi”

“Aha…hapo nina swali, hizo CD, zitaua vipi kifaa cha mnunuzi?”

“Kwa mfano kwa wale ambao wamezoea kununua CD moja kisha anakwenda kuzalisha ma CD mengi sana na yeye anauza kwa watu labda kwa bei ya chini, basi mtu kama huyo ategemee kwamba hicho kifaa atakacho kuwa anajaribu kuhamishia filamu yetu na kuingai kwake kitakufa.”

“Kwa kutazama je?”

“Kwa kutazama hiyo haina shida kabisa, anaweza kutazama hata mara mia CD moja pasopo kuingia michubuko ya aina yoyote wala kukwama kwama”

“Niliweza kujadiliana na meneja wa masoko akaniambia kwamba kuna mkataba ambao mkurugenzi muliingia na kampuni ya Universal katika swala la usambazaji”

“Ndio”

“Basi itabidi tuweze kukaa nao chini na tuweze kujadiliana juu ya siku ambayo tunaweza kuiachia filamu hii ili na wao wenyewe waanze kuweka trela ya hii filamu kwenye akaunti zao za mitandao ya kijamii”

“Sawa, je tunaweza kuiona filamu?”

Swali langu kama likampa kigugumizi dokta Clara cha kujibu. Tude Class akasimama.

“Hapana madam, bado sijaifanyia final editing”

“Ahaaa sawa sawa”

“Na kama huto jali madam Jojo, ningeomba uweze kushirikiana nami katika kufanya final Editing, kama kutakuwa na kitu cha kupunguza na kuongeza tunaweza kukifanya”

“Sawa”

“Nakaribisha maoni jamani”

Akasimama dada mmoja aliye valia sketi ndogo fupi na shati la mikono mirefu huku akiwa amechomekea vizuri.

“Aahaa kwa mimi napenda nishauri kitu kimoja, kwa zile filamu ambazo zimerekodiwa tayari, ningeomba ziweze kupitiwa nazo ili kama zitakuwa na mapungufu tuweze kuziona”

“Asante wa jina, ila hizo filamu tulizo zirekodi tutaziwekea siku yake ambayo tunaweza kuzitazama ila kwa sasa tuangalie hii filamu yetu ambayo inaweza kwenda kuzindua kampuni yetu”

Dokta Clara alizungumza kwa upole.

“Clara zina trela zake?”

“Mbili zinazo”

“Hembu tuzione”

Hapakuwa na namna zaidi ya wao kufwata kile ninacho kizungumza. Tukaanza kutazama filamu ya kwanza, kusema kweli kutoka moyoni sijaipenda kabisa, kwani ni filamu ambazo hazitofautiani kabisa na zinazo tengenezwa na wasanii wa kawaida sana.

“Hii filamu story yake imenadikwa na nani?”

“Mimi hapa mkuu”

Kijana mmoja alizungumza huku akinyoosha mkono, kwa bahati nzuri yupo mbele yangu.

“Hembu ni elezee hiyo hadithi inahusiana na nini?”

“Ahaaa, yaani hiyo hadithi kuna mzee mmoja yupo kijijini, yeye ni mchawi sana. Sasa alikuwa na binti yake wa kike, watu walikuogopa sana yule binti na mwishowe vijana wakaamua kumbaka, kwa bahati mbaya walivyo mkaka yule binti alikufa, mzee sasa akaamua kuhakikisha kwamba anaua kijiji kizima kwa kukiroga”

“Baada ya kuwaroga?”

“Filamu inahishia hapo”

Nikajikuta nikitabasamu na wafanyakazi wote wananitazama.

“Kwa hiyo mzee huyo mchawi ndio muhusika mkuu wa filamu?”

“Ndio madam”

“Hiyo ni story yako ya ngapi kuandika?”

“Yaa nne na zote naamini ni kali madam”

“Kabla sijatoa maoni yangu, hembu jamani nisaidieni kwa maoni yenu, kuweni wawazi na wala musiwe na wasiwasi kabisa wa kutoa maoni”

Kijana mmoja mtanashati akanyoosha mkono juu.

“Ndio”

Taratibu akasimama na kutufanya sote tumtazame.

“Kusema kweli madam, kwa filamu ambayo umecheza wewe na kuiweka hii tuliyo toka kuona trela yake kusema kweli ni utumbo, tena utumbo wa kuku”

Watu wote tukajikuta tukicheka, ila kijana mwenye story yake akaonekana kuchukizwa na maneno hayo.

“Kusema kweli, kwanza stori ni mbaya, wahusika kidogo wamejitahidi ila kilicho fanyika hapo ni ubabaishaji kwa kweli. Asante”

“Ehee mwengine”

Akasimama msichana mmoja mrefu kiasi na mwembaba kwa kumbukumbu zangu za haraka ndio msichana aliye igiza kama mjukuu wa mzee huyo mchawi.

“Ahaa mkuu hapo labda mimi nimkosoe Jose. Kitu ambacho kinaendelea kati ya Jose na William ni kwamba wana bifu, tena bifu lenyewe la kugombania msichana ndio maana anasema kwamba filamu sijui ni utumbo wa kuku. Filamu ni nzuri tena nzuri sana. Mule ndani waigizaji wamefanya vizuri kwa kweli, kama ni uongo watu wasema, filamu hii kama ni kali au si kali”

“Dada unaitwa nani?”

“Pili?”

“Asante pili kwa maoni yako. Mwengine”

Akasimama mama mmoja ambaye kidogo kwa kumtazama anaweza kufika kwenye miaka arobaini na kitu hivi.

“Kwanza ninafurahi kukutana na wewe Jojo. Ahaa kitu kingine cha pili hii story kusema kweli ni nzuri hata mimi nampa big up sana Wiliam, story zake ni nzuri nzuri sana sijaona za kufananisha naye ukitoa tu muandishi wa hiyo filamu uliyo cheza. Asante”

“Asante mama, mwengine?”

Akasimama kijana ambaye ninakumbuka alisha wahi kunitongaza siku ambayo tulipo kuwa tunasherekea kumaliza kumaliza kutengeneza filamu ya Love Mask.

“Jamani kusema kweli nahitaji kuzungumza kitu ambacho nina imani kitawakera wengi na kuwaboaa wengi, ila ukweli ni ukweli.”

“Katika filamu hii kusema kweli hakuna kitu kilicho weza kufanywa, kuanzia uandishi hadi uigizaji. Kwa nini ninasema hivyo, lengo la kampuni ni kuhakikisha kwamba tunafanya mapinduzi katika soko la filamu hapa Tanzania, Afrika na dunia kwa ujumla. Ila kwa mfumo wa story hizo zisozo na mwisho mzuri, kusema kweli tumebugi, nakumbuka William nilikuambia tangu ulipo kuwa unailete filamu hii mezani tuijadili na watu waingie location, nikasema jamani hii filamu ya kurekodi waiki moja au mbili sio filamu, tunabugi, ila watu wote humu ndani mulichukia na kila mtu alizungumza lake. Nilikuwa nikiongea vile kwa maana najua ni kitu gani ambacho alikifanya director wa filamu ya kwanza kaka yangu Eddazaria. Filamu ya love Mask ilitugarimu kama miezi saba au nane hivi hadi kuisha, ila hiyo ya mzee wa kijijini, imetugarimu wiki moja wapi na wapi jamani. Mkuu yangu ni hayo tu”

“Nashukuru kwa maoni, mwengine”

Akasimama mzee mwengine mwenye kitambi.

“Ahaa naitwa bwama Marcus, ni meneja masoko. Kusema kweli hiyo filamu mkuu ina weza kufanya vizuri sana, hivyo ninaomba tuweze kuipa nafasi. Asanteni”

Mzee huyu mara baada ya kukaa nikanyanyuka, nikajiweka vizuri dera langu.

“Jamani nimeyasikia maoni yenu. Clara filamu hiyo imeweza kugarimu kiasi gani hadi kufaa?”

“Ahaa, muhasibu, naomba ujibu swali”

Kijana mmoja alisimama huku akitabasamu.

“Imegarimu kiasi cha milioni themanini”

Nikajikuta nikiguna kimoyo moyo.

“Hadi kumalizika?”

“Ndio”

“Kamera, usafiri vyote ni vya kampuni?”

“Ndio mkuu?”

“Watu walikaa kambi siku ngapi?”

“Wiki moja na siku nne”

“Sawa na siku kumi na mbili”

“Ndio mkuu”

“Milioni hiyo themanini imetumika kwenye nini?”

“Kulipa wasanii, kulipia makazi ya kijijini pale na chakula?

“Wasani walikuwa wangapi?”

“Eheee?”

Kijana huyo mwili ulianza kumtetemeka hata sauti yake nayo ikatawaliwa na mitetemesho.

“Umenisikia?”

“Tulio toka nao huku Dar walikuwa hamsini na tano, na…na na tulio wakuta kule walikuwa walikuwa wangapi vile?”

“Hamsini pia?”

“Msanii aliye lipwa kwa kiwango cha juu ni shilingi ngapi?”

“Milioni mbili na nusu mkuu?”

“Aliye lipwa kiwango cha chini?”

“Elfu tano?”

“Elfu tano!!?”

“Ndio mkuu”

“Clara niitie walinzi wangu, ninaondoka na huyu kijana, humuwezi kunifanyia ujinga na wizi wakipuuzi kwenye kampuni yangu alafu niwachekee kwa upuuzi wa filamu ya kiseng** kama hiyo. Hamjui ni mangapi nilipitia na ninaendelea kupitia kulinda hii kampuni, sitaki ukinga kabisa”

Nilizungumza kwa hasira sana hadi nikajikuta tumbo likianza kuniuma taratibu na jasho jingi likaanza kunimwagika usoni mwangu.


Judy kwa haraka akanyanyuka kwenye kiti chake na kunifwata nilipo kaa, akanishika mkono na kuninyanyua. Tukatoka ndani ya ukumbi huu na kuingia ofisini kwangu.

“Jojo kumbuka mama amekuambiaje lakini, mbona unataka kujitafutia matatizo na hali yako hii, au unataka mimba itoke ehee?”

Judy alizungumza kwa msisitizo huku akinitazama usoni mwangu.

“Ila hawajui mateso niluyo pitia hadi leo kuwa hapa”

Mlango ukafunguliwa, akaingia dokta Clara.

“Clara tupishe kwanza”

Judy alizungumza huku akimtazama dokta Clara. Clara akatoka ofisini humu na kutuacha sisi wawili.

“Hata kama, ila tazama hali yako, tazama kiumbe kilichopo tumboni mwako. Hicho ndio muhimu kuliko hata hii kampuni sawa”

Judy aliendelea kuzungumza kwa msisitizo, nikaka kimya huku nikiyasikilizia mapigo yangu ya moyo jinsi yanavyo nienda kasi.

“Tazama sasa, jesho linavyo kumwagika na humu ndani kuna A/C ya kutosha”

“Ngoja nikamalizie kikao”

“Hapana hakuna kwenda sehemu yoyote, tunakwenda nyumbani sasa hivi?”

“Siwezi kwenda nyumbani?”

“Nakuambia tunakwenda nyumbani Jojo, sitaki matatizo saa hivi. Unajua ni kiasi gani nilikuwa ninalia kwa ajili ya kukuombea wewe, eheee?”

Judy alizungumza huku machozi yakimlenga lenga usoni mwake. Nikaka kikmya huku nikijaribu kushusha hasira yangu. Nikanyanyuka kwenye kiti nilicho kikalia, nikaelekea mlangoni kabla sijafika Judy akanishika mkono.

“Unataka kwenda wapi?”

“Nyumbani”

Tukatazamana na Judy kwa muda kisha akaniachia, akafungua mlango na tukatoka humu ndani na kumkuta dokta Clara akiwa amesimama nje ya mlango wa ofisi yetu, huku kukiwa na walinzi wawili.

“Mumemchukua?”

“Hapana tunasubiria maamuzi yako”

“Mchukueni na mumuweke chini ya uangalizi na mahesabu ya pigwe, fwatilia kila shilingi mia, kama kuna pesa yoyote imtumika kiholelea, nahitaji ziweze kurudishwa la sivyo atazungumza na mahakama sawa”

“Sawa”

“Niletee pochi yangu”

Dokta Clara akaingia ndani ya ukumbi wa mikutano, baada ya muda akarudi akiwa ameshika pochi yangu, akamkabidhi Judy.

“Clara nakuamini na ninahitaji hili jambo lifwatiliwe, wewe si ndio meneja?”

“Ndio”

“Sasa mambo yakienda kombo sinto kuwa na huruma na hata wewe mwenyewe”

“Nimekuelewa, na ninakuhidi kwamba kila kitu nitakisimamia na hakuna jambo ambalo litakwenda hovyo”

“Sawa”

Nikaongozana na walinzi wangu hadi kwenye lifti. Tukaingia na mlinzi wangu mmoja akaminya batani ya gorofa ya chini kabisa.

“Inabidi nijifunze na mimi maswala yako ya kuogoza kampuni”

Judy alizungumza na kunifanya nimtazame usoni mwake kwa macho ya kumdadisi na sikumjibu kitu cha aina yoyote zaidi ya kukaa kimya. Tukafika chini, lifti ikafunguka na kuwakuta walinzi wangu wengine wakiwa wanatusubiri. Kundi kubwa la waandishi wa hahabri likaanza kutuzonga zonga, na wala sikujua wametokea wapi. Kila mwandishi anatamani japo nimjibu swali langu ila walinzi wangu wapo makini sana katika kuhakikisha kwamba hakuna mundishi wa habari anaye weza kunigusa hata dera langu.

“Tunasikia Eddazaria amekufa?”

Swali la muandishi mmoja aliye liuliza akiwa nyuma yangu likanifanya nisimame, nikamgeukia na kumtazama kwa macho makali sana.

“Dada twende bwana”

“Wewe ndio umemuua au?”

Niliuliza kwa ukali huku nikimtazama mwandishi huyu.

“Tungependa kujua amekufaje kufanye na mbona hakuna mazishi yake”

Judy akanishika mkono na tukaendelea kueleka yaliyo magari yetu. Mlinzi akanifungulia mlango na nikaingia, kisha akaufunga na Judy akazunguka upande wa pili na kuingia ndani ya gari. Machozi yakaanza kunimwagika huku wandishi wa habari wakiendelea kutupiga picha.

“Usijlie bwana dada, kwani hilo jambo halina ukweli wowote”

“Ila sipendi mume wangu azungumziwe vibaya bwana”

“Najua unajua kwamba huwezi kuwazuia wanadamu kusema. Sikuzote wanadamu wameumbwa kwa ajili ya kuzungumza”

Judy aliendelea kunibembeleza huku tukiondoka eneo hili.

“Yule aliye kupigia simu alikuwa ni nani?”

“Wala hakuzungumza kabisa zaidi ya kukaa kimya”

“Mmmm hembu niiangalie hiyo namba kwa maana mimi sijawahi kumpigia mtu simu kwa hiyo namba niliyo kupatia”

Nikamkabidhi Judy simu yangu akaitazama namba hii kwa umakini, kisha akaguna.

“Vipi?”

“Namba hii ya nchi gani?”

“Hata mimi sifahamu?”

“Ulijaribisha kuipiga?”

“Wala sikuipiga”

“Ngoja niipige”

“Kwa kutumia laini yangu?”

“Ehee, kwani si imepiga kwenye laini yako”

Judy akafanya kama alivyo dhamiria kisha akaweka loudspeaker na kutufanya sote tusikie. Lugha ya kama muhudumu wa kike anaye zungumza, haikuwa kingereza, kichna wala Kiswahili, ni lugha ambayo kusema kweli ndio mara yangu ya kwanza kuzungumza.

“Ndio lugha gani?”

“Ni kirusi”

Mlinzi wangu alijibu.

“Kirusi ndio lugha gani?”

Judy aliuliza huku sote tukimzatazama mlinzi huyo wa kike.

“Kuna inchi inaitwa Russia, hiyo ndio lugha wanayo izungumza”

“Ahaaa, hapo sasa tumekuelewa, sasa huyu dada anamaanisha nini?”

“Ahaa, yaani ni sawa na pale unapo gia simu na mtu akakukatia simu. Huwa si unasikia kwamba namba unayo ipiga kwa sasa inatumika?”

“Ehee?”

“Ndio maana yake sasa”

“Ahaa, kwa hiyo tuliye mpigia amekata simu”

“Ndio”

“Sasa huyo aliye piga hii namba ameitoa wapi, au wewe utakuwa kuna mtu umempatia hii namba?”

“Yaani sijampatia mtu wa aina yoyote namba, kwa siku hizi ulizo kaa nayo ni nani na nani ambao uliwasiliana nao kwa hiyo namba”

“Mmmmm, kuna wifi, na shem tu ndio niliwasiliana nao”

“Hao wawili tu?”

“Ndio na nina imani kwamba wao hawawezi kuitoa namba yangu kwa mtu mwengine pasipo idhini yangu”

“Mmmm, hapo kuna kitu nina kihisi”

“Kitu gani?”

“Sio shemeji kweli huyu”

Nikamtazama Judy kwa muda huku nami machale yakianza kunicheza, kama namba yangu anayo wifi na shem, na kama kweli Eddazaria atakuwa yupo hai, basi wao hawawezi kumnyima mdogo wao namba yangu, isitoshe nimejaribu kuwauliza kwa mara kadhaa kuhusiana na ukweli wa kutoweka kwa mume wangu ila hakuna kati yao aliye weza kunipa jibu la kuuridhisha moyo wangu.

“Eti dada kuna mtu yoyote anaye jua juu ya kutoweka kwa Eddy?”

Niliwaula walinzi nilio kuwa nao ndani ya hili gari, dada ambaye alizungumza nasi akanigeukia na kunitazama kwa sekunde kadhaa kisha akatingisha kichwa akimaanisha kwamba hajui kabisa.

“Kweli hufahamu?”

“Ndio”

Nikamkazia macho dada huyu, yeye mwenyewe akajikuta akitazama mbele, kwa haraka haraka ni mtu ambaye anaweza kufahamu ni kitu gania ambacho kinaendelea, ila anasita kuzungumza. Nikajukausha kimya huku nikimya. Hadi tunafika nyumbani sikuzungumza kitu chochote. Tukashuka kwenye gari, tukamkuta mama mkwe akiwa amesimama eneo la juu y agora ambalo kuba sehemu ya kupumzikia.

“Nahitaji kuzungumza nawe”

Nilimuambia dada huyu.

“Sio kwa sasa hivi kwa maana mkuu yupo”

Mlinzi huyu alizungumza huku akinionyeshea kwa ishara ya macho katika eneo ambalo amakaa mama mkwe.

“Sawa”

Nikamuacha huku nikielekea ndani.

“Judy nataka tuitafute namba hii ili tuweze kufahamu ni nani ambaye anaitumia”

“Tutaitafuta vipi?”

“Kwenye mtandano”

“Mmmm kuna rafiki yangu mmoja hivi wa kihindi, yupo Tanzania hapa, yeye amesomea maswala ya I.T, sijui nini huko, nahisi kwa kupitia yeye anaweza kutusaidia”

“Ni mwanamke au mwanaume?”

“Mwanamke, nilikuwa naye kule hospitalini, seme yeye alikuwa ana muuguza mama yake”

“Unaweza kuwasiliana naye akaja huku mara moja”

“Ngoja nijaribu”

“Fanya hivyo basi alafu unipe jibu”

Nilizungumza huku nikipandisha ngazi kuelekea gorofani. Nikakutana na mama mkwe kwenye kordo

“Vipi best huko mulipo toka kwema?”

“Kwema mama, nimeweza kuona mabadiliko uliyo yafanya”

“Yaa ni kweli japo sina utaalamu sana na maswala yenu ya filamu, ila ili niweze kuokoa kile ambacho mumekianzisha nikaonan ni vyema kuweka mfumo wenye usimamizi mahiri utakao wasaidia hata kama mukiwa hamupo”

“Ninashukuru sana mama kwa maana ni kazi nzuri umeifanya japo nimekuta kuna madudu kadhaa wafanyakazi wameyafanya ila nitaendelea kuyapunguza taratibu taratibu”

“Akhaa, wamesha anza kufanya madudu?”

“Si unajua tena waswahili mama yangu”

“Ahaa, haya nimekuandalia mtori fanya ukale kwa maana ni mchana sasa”

“Sawa mama yangu, ila nahitaji kupumzika kidogo”

“Mmmmm….kula kwanza kisha ndio upumzike”

“Sawa”

Ikanilazimu kushuka ngazi na kwenda jikoni, nikajimiminia mtori huu kwenye bakuli kangu kubwa, nikakamulia ndimu nyingi kisha nikalibeba na kueleka chumbani kwangu. Judy akaingia huku akiwa amejawa na tabasamu.

“Nini?”

“Amesema anakuja”

“Basi unatakiwa ukae hapo getini, si unafahamu ulinzi umeimarisha, isije akashindwa kuingia humu ndani”

“Sawa anasema amatuona kwenye tv leo”

“Wamesha irusha habari yetu?”

“Ndio”

“Hembu washa hiyo Tv”

Judy akawasha tv, tukajaribu kutazama kwenye vituo vya televishion baadhi baadhi vya nchini hapa Tanzania ila hatukuweza kuona kitu chochote.

“Mtoto akizaliwa atakuwaje bonge, kwa maana una fukia kishenzi”

“Kwenda zako, sasa unataka nizae njiti”

“Mmmm ila angalia mtoto asije akawa na kile nyingi ukapigwa kisu, hapo ndipo ubovu utakapo anzia”

“Hembu bwana na wewe nitolee maneno yako ya kishetani, badala ya kuniombea unaanza kuniambai sijui nikapigwa kisu, sasa wewe tafurahi nikizaa kwa oparesheni au?”

“Hapana, ila nisamehe kama nimekuudhi, naona umesha anza kukasirika na jasho lako la hasira limesha anza kukutoka”

“Sipendi maneno ya kijinga”

“Jamani si nimeomba msamaha jamani, hiyo mimba yako inakufanya uwe na mahasira Jojo, au hujaligundua hilo swala?”

Kabla sijamjibu Judy kitu cha aina yoyote simu yake ikaanza kuita, akaipoke na kuiweka sikioni mwake.

“Ahaa umefika”

“Nakuja sasa hivi”

Juduya akaka simu yake na kushuka kitandani tulipo kaa, akatoka nje na kuniacha nikiendelea kunywa vijiko vya mtori huu taratibu. Baada ya muda akaingia chumbani humu akiwa ameongozana na binti mwenye hasili ya kiindi. Binti huyu akanisalimia kwa furaha sana nani nikatabasamu ili kumkarimu, akatoa laptop yake na kuiweka juu ya meza.

“Ulisha mueleza nini tunahitaji?”

“Ehee, Judy amesha nieleza”

Msichana huyu akaanza kiminya minya batani zake mimi na Judy kazi yetu ni kukodoa macho tu kuangalia anacho kifanya huyu msichana. Baada kama ya dakika tano hivi akatutazama kwenye nyuso zetu.

“Vipi umefanikiwa?”

Niliuliza huku nikiwa na shauku kubwa ya kuhitaji kufahamu ni nini kinacho endelea.

“Ndio”

Alijibu kuhu akitugeuzia laptop yake na tukaangalia. Jina la mtumiaji wa namba ya simu aliyo kabidhi na Judy, anaitwa Omary Macovic, yupo Mosscow Russia. Kazi yake ni mwanajeshi anaye jifunza mafunzo ya ukomandoo.

“Mmmmm sio yeye”

Judy alizungumza kwa upole huku akishusha pumzi nyingi sana.

“Tunaweza kuiona sura yake”

“Ndio”

Binti huyu akaminya batani moja, taratibu picha ya mtu huyu ikaanza kufunguka kwa kufutika futika, macho yakanitoka, jasho likaanza kunimwagika mwilini mwangu, kwani mtu ninaye muona hapa si mwengine bali ni mume wangu Eddazaria, na huku amevalia mavazi ya kijeshi ya nchi hiyo pamoja na kofia nyekundu ya kijeshi. Swali linalo niumiza kichwa, amefikaje fikaje huko Russia na imekuwaje amebadilisha jina na kujiita Omary Macovic.



Ukimya ukatawala kati yetu, Judy akanitazama kwa macho yaliyo jaa mshangao. Nikajificha jasho linalo nimwagika usoni mwangu. Nikashusha pumzi nyingi sana ili kuyaweka sawa mapigo yangu ya moyo ambayo yananienda kwa kasi. Kusema kweli hili jambo nililo liona hapa lime nishangaza na kuniduwaza.

“U..ume…sema yupo wapi?”

“Yupo Mosscow”

“Ni lazima niende Russia”

“Jojo……!!!”

“Nini, ni lazima niende kumtafuta mume wangu, unajua ni matatizo ya aina gani ambayo nina yapitia katika moyo wangu, unaniona sasa hivi mstuko mdogo tu jasho lina nimwagika, hapo awali sikuwa hivyo”

Nilizungumza kwa msisitizo huku nikishuka kitandani, bakuli langu lenye mtori kidogo nikaliweka mezani.

“Jojo, nakuomba unisikilize, hujui huko labda shem amekwenda kufanyeje nakuomba uweze kutulia basi tutajua ni nini cha kufanya kuliko kukurupuka”

“Judy katika hili si wewe, si nani anaweza kunizuia sawa, na kama upo upande wangu na ni mdogo wangu tuliye zaliwa tumbo moja ninakuomba uweze kushirikiana nami katika hili. Ukikataa tambua fika kwamba wewe sio ndugu yangu sawa”

Maneno yangu yakaonyesha kuwa makali sana kwa Judy, kwani machozi usoni mwake yakaanza kumlenga lenga. Nikafungua kabati kubwa la nguo, nikafungu kiji droo kidogo kilichomo ndani ya kabati hili na kukuta hati yangu ya kusafiria inayo weza kuniruhusu kwenda nchi yoyote dunia pasipo kipingamizi cha aina yoyote.

“Jojo unataka kuondoka sasa hivi?”

“Ndio”

“Nakuomba unisikilize hili swala nahitaji tulifanye siri, kama wao walivyo fanya siri kukuficha ni wapi alipo mume wako. Usionyeshe utofauti wa aina yoyote katika hili, tulia tusuke mipango ya kukufanya uweze kwenda huko Russia pasipo kufanya hivyo utajikuta ukikaa katika kifungo cha ndani kwa maana ninahisi unajua ukali wa mama mkwe wako”

Maneno ya Judy kidogo yakaanza kuniingia akilini mwangu, kwani ni kweli mama yangu mkwe hapendi kabisa niwe ninatoka hata nje ya geti la nyumba yangu na ndio maana ameniweka walinzi wengi kupindukia.

“Tulia Jojo, acha nikuandalie mazingira ya wewe kwenda huko Russia, kuna mdada nina mfahamu yupo kwenye shirika la ndege ya Russia, nitamtafuta nizungumze naye akuandalie mazingira mazuri sawa”

“Una uhakika na hicho unacho kizungumza?”

“Asilimia mia moja, nipe siku mbili, siku mbili tu zitanitosha”

Nikamatazama Judy usoni mwake, kisha taratibu nikamkumbatia, kwani huyu ndio mtu wa pekee kwa sasa ninaye weza kumuamini katika swala hili kwani hata mama Eddazaria mwenyewe amenidanganya juu ya wapi alipo mwanye na huniambia siku zote kwamba bado wanaendelea kushuhulikia kuchunguza ni wapi alipo mwanaye.

“Nakupenda sana Judy, na nina kuamini mdogo wangu”

“Nakupenda pia dada, msaada wako ulio weza kunipatia kipindi nilipo kuwa nimetekwa na kina Chibidu, siwezi kuusahau, nahisi hadi leo ningekuwa nimesha kufa, hadi leo nahisi ningekuwa ni marehemu”

“Nashukuru”

“Rani, unaweza kutusaidia kumtafuta zaidi huyo mtu”

Judy alizungumza huku akimtazama binti huyu wa kihindi hapa ndipo nikagundua kwamba jina lake anaitwa Rani.

“Yaaa na weza”

“Hembu”

Tukarudi tena kitandani, alipo keti Rani, akaendelea kuminya minya batani za laptop yake, kutokana sisi hatujui nini anafanua, tumekuwa mashahidi wa kutazama anacho kitenda.

“Ahaa…hana histiria yoyote wala picha nyingine zaidi ya hii?”

“Huwezi kutafuta tafuta na kujua ni nyumba gani anayo ishi?”

“Hapana nimeshindwa, watu kama hawa ni ngumu sana kuweza kufahamu ni wapi wanapo ishi, kwa maana maisha yao yanakuwa ni ya siri”

“Ila kutokana tumefahamu kwamba anapatikana Mossow basi haina tabu, ukienda tutajua ni kitu gani cha kufanya”

“Sawa, Rani naomba pia iwe siri kwa upande wako”

“Wala usijali Jojo, tuliyo yajadili yataishia humu humu ndani”

“Kweli?”

“Ndio”

“Tunashukuru kwa hilo”

Mlango ukagongwa, kwa haraka Judy akaniletea bakuli langu la mtori na kunikabidhi.

“Ingia”

Nilizungumza kwa suati ya upole. Mama mkwe akaingia ndani humu.

“Vipi best?”

“Safi mama”

“Hadi sasa bado hujamaliza tu kunywa mtori”

“Namalizia mama yangu”

“Sawa, mimi ninatoka, ninaelekea Ubungo kumuona mjomba mara moja”

“Ahaa sawa mama?”

“Judy muangalie mwenzio, na ikifika jioni hakikisha unafanya mazoezi madogo madogo”

“Sawa mama”

“Haya mubaki salama”

Mama mkwe akatoka chumbani humu, Judy naye akatoka.

“Hembu naiomba ile picha ya Eddy unitumie Whatsapp”

“Sawa”

Rani akafanya kama nilivyo muagiza akanitajia namba yangu ya WhatsApp kisha nika akanitumia. Nikaanza kuikagua picha hii, ya mume wangu mtarajiwa, nikajikuta machozi yakinitoka usoni mwangu kwa furaha. Mlango ukafunguliwa, akaingia Judy huku nyuma yake akifwatwa na mlinzi wa kike ambaye tulikuwa naye kwenye gari.

“Mama amesha ondoka?”

“Ehee, ameondoka na baadhi ya walinzi”

“Ok. Dada karibu”

“Asante”

“Kuna mswali nitakuuliza, ninakuomba uweze kunijibu kiufasaha”

“Sawa ulizi, nikiwa nina yafahamu nitakujibu, ila nikiwa siyafahamu nitajiri kwamba sifahamu”

“Umefahamu ni wapi alipo Eddy?”

Dada huyu akaka kimya huku akinitazama usoni mwangu.

“Hei?”

“Eehhee?”

“Unafahamu ni wapi alipo Eddy”

“Hapana”

“Acha kuniongopea, macho yako dhairi yanaonyesha kwamba unafahamu. Tafadhali nakuomba uwe muwazi, na kuomba uwe mkweli katika hili”

Nilizungumza kwa msisitizo na kumfanya dada huyu kushusha pumzi.

“Najua upo kazini, natambu ni ngumu kwa mtu kuweza kitoa siri za kazi yake, niambie ukweli kupitia hili nakuhakikishia kwamba maisha yako yanakwenda kuwa mazuri. Tafadhali nakuomba uweze kuniambia ukweli”

Dada huyu akavua kifaa malumu cha mawasiliano alicho kichomeka sikioni mwake, kisha taatibu akakaa pembeni yangu.

“Nakuomba iwe ni siri kwa maana naitegemea hii kazi”

“Kwani unalipwa kiasi gani?”

“Milioni mbili na nusu”

“Nitakulipa milioni tano kila mwenzi na ninahitaji uwe mlinzi wangu, utakaye beba siri yangu nami nitabeba za kwako.”

Dada huyu akashusha pumzi nyingi huku akinitazama usoni mwangu.

“Niamini”

“Kweli muamini dada yangu huwa haongopei kabis akwa kile ambacho anakizungumza”

Judy naye aliweka msisitizo ulio mfanya dada huyu kuendelea kukaa kimya.

“Aha..ninacho kifahamu mimi….”

“Eheee”

“Mume wako yupo hai”

Nikajiweka vizuri kitandani ili niendelee kusikiliza ni kitu gani atakacho kizungumza huyu dada.

“Sifahamu ni wapi alipo ila ninafahamu kwamba yupo hai?”

“Ile namba tuliyo kuwa tunaipiga inaonyesha kwamba muhusika ni huyu hapa”

Nikamgeuzia dada huyu laptop na kumuonyesha picha ya Eddazaria.

“Nina imani umesha mfahamu”

“Ndio”

“Kwa sasa yupo nchini Russia, katika mji wa wapi vile?”

“Mosscow”

Rani alinisaidia kulijibu hilo.

“Sawa”

“Nahitaji kwenda huko”

“Russia?”

“Ndio”

“Hilo swala ni gumu sana”

“Ndio ni gumu sana ila kupitia wewe litakuwa ni rahisi”

“Siwezi kuifanya kazia mbayo itaniweka maisha yangu hatarini na jua pesa ni muhimu ila usalama wangu pia ni muhimu kuliko chochote kwa manaa nina tegemea na nina familia ya mtoto mmoja na mume”

Dada huyu alizungumza huku akisimama.

“So huwezi kunisaidia?”

“Kwa kwenda Russia sinto weza, samahani kwa hilo”

Dada huyu akaanza kutembea kuelekea mlangoni.

“Unaonaje nikakupatia milioni kumi kwa mwenzi”

Dada huyu akasimama mlangoni kwa muda huku akiwa ameshika kitasa cha mlango huu. Akanigeukia na kunitazama usoni mwangu.

“Samahani hata iwe milioni mia moja siwezi kuifanya hiyo kazi. Asante”

Dadada huyu akafungu mlango na kutoka chumbani humu.

“Mmmm ana jishaua naye”

Judy alizungumza huku akifunga mlango kwa ndani.

“Mtafute basi huyo dada unaye mfahamu?”

“Yule ni hadi nitumie Whatsapp kuchati naye”

“Fanya hivyo basi”

Judy akaichukua sikmu yake na kuanza kumtafuta dada huyo. Nikaichukua simu yangu na kumpigia dokta Clara. Simu yake ikaita baada ya muda ikapokelewa.

“Haloo”

“Clara ni mimi”

“Niambie Jojo”

“Upo wapi?”

“Bado nipo ofisini, tunaendelea kufwatilia mtiririko wa matumizi ya pesa na kweli mapungufu yapo”

“Okay hivi kwa hali kama hii yangu ninaweza kufanya kazi au kusafiri kwa muda mrefu?”

“Kwa ujauzito wa miezi miwili ndio ina wezakana kusafiri kwa muda mrefu”

“Ok sawa, je una fahamu chochote kuhusiana na nchi ya Russia?”

“Mmmmm mimi nninaiona tu kwenye video na kuisoma kwenye ramani tu”

“Ahaa, kwa hiyo hujui chochote?”

“Yaa kuwa muwazi sifahamu chochote”

“Poa badae”

“Haya”

Nikakata simu na kumgeukia Judy

“Nachati naye na anasema kwamba leo hii wapo Tanzania na wanaondoka hapa saa tisa usiku”

“Saa tisa usiku”

“Ndio ndege yao ndio inaondoka, nimemuomba aweze kuniwekea siti moja”

“Kwa…kwa hiyo unataka niondoke usiku wa leo?”

“Ndio Jojo hii ndio nafasi ya kwenda kumtafuta mume wako kama kweli una mpenda, hatuna nafasi nyingine kwa maana dada huyu anaseama hii ndio itakuwa safari yake yeye ya mwisho kuwepo Tanzania”

“Una maana gani ni safari yake ya mwisho”

“Anahamishiwa kwende ndege zitakazo kuwa zinatoka Russia kwenda nchini Marekani na huko hato kuja tena”

Maneno ya Judy yakanifanya nikae kimya kwa muda huku nikitafakari ni namna gani ninaweza kufanya ili ktoroka katika nyumba hii na kuelekea nchini Russia kumtafuta mume wangu kipenzi Eddazaria.



“Jojo pambana kwa ajili ya penzi lako. Usikubali kumpoteza mume wako”

Maneno ya Judy yakazidi kunge ushahidi kwenye akili yangu. Hamu na hamasa ya kwenda kumtafuta Eddazaria huko alipo japo hadi sasa hivi sifahamu ni sababu gani za msingi zilizo pelekea hadi yeye kupelekwa au kwenda nchini Russia.

“Niandakie nguo zangu kwenye kijibegi kidogo kile cha mgongoni, na nenda benki sasa hivi ukanitolee dola elfu ishirini”

“Nahisi ninazo”

“Unazo ndani?”

“Ndio”

Nikatamani kumuuliza ametoa wapi kiasi chote cha pesa hizo ila nikaka kimya kwa maana lengo lililopo sasa hivi ni kuhakikisha kwamba ninaondoka nchini Tanzania pasipo mama mkwe wala walinzi alio niwekea kuweza kufahamu.

“Sasa hivi ni saa ngapi?”

“Ni saa kumi na moja kasoro”

“Na ndege inaondoka saa ngapi umesema?”

“Saa tisa usiku”

“Na ameweza kukuambia kwamba ameandaa tayari tiketi ya ndege??”

“Ndio na visa tayari amesha kukatia”

“Visa ya muda gani?”

“Ameniambia niya mwezi mmoja”

“Poa, sasa uwanja wa ndege nitaendaje kwa maana hapa siwezi kutoka na gari”

“Mmmm hapo ndipo kazi ilipo”

“Na muda ninao toka utakuwa ni usiku sana”

Sote tukaka kimya huku tukiwaza ni kitu gania mbacho tunaweza kufanya juu ya usafiri ambao utanipeke uwanja wa ndege.

“Mimi ningewasiaidi ila kwetu ni mbali na muda huo sidhani kama nitaweza kutoka nyumbani”

Rani alizungumza huku akitutazama kwenye nyuso zetu.

“Kuna mtu nime mkumbuka”

Nilizungumza huku nikimkumbuka bodaboda wa kwanza kabisa ambaye alikuwa akinitembeza maeneo mbali kipundi nilipo kuwa nilipo kuwa ninahamia huku.

“Nani?”

“Kuna bodaboda mmoja anaitwa Jofu nilisha wahi kumtumia kipindi cha nyuma sana, sijui atakuwa bado yupo eneo hili au amesha hama”

“Anapatikana wapi?”

“Pale kwenye kituo pale barabarani wanapo simama bodaboda”

“Ndipo anapo patikana?”

“Ndio”

“Ngoja nikamcheki”

“Wewe ukifika pale ulizia Jofu, utampata tu”

“Yupoje poje?”

“Si mfefu wala mfupi, ni mwembaba kiasi na anapenda kuvaa kofia zinazo kuja mbele hivi?”

“Cape?”

“Ehhheee hizo hizo”

“Poa”

“Ukifika wewe chukua namba yake sawa”

“Sawa”

Judy akachukua mtandio na kujifunika kichwani, kwa yeye nina imani huwa hasumbuliwi kwenye swala zima la kutoka katika uzio wa jumba hili.

“Jojo”

Rani aliniita kwa sauti ya upole huku akinitazama usoni mwangu.

“Ehee”

“Kwenda Russia, nina hisi kwa upandw wangu sio maamuzi mazuri”

“Kwa nini?”

Nilizungumza huku nikimdadisi sana Rani.

“Tumefahamu kwamba mume wako yupo Russia, ila hatuna uhakika na eneo alipo, ni sawa na mtu akakuamia anaishi hapa Dar es Salaam alafu haujui ni wapi anapo ishi, ikiwa kuna Kijitonyama, Tabata, Mbagala, Mbezi na meneo mengine mengi ambayo sio rahisi kuweza kujua ni wapi anapo ishi”

“Unahitaji nisiende?”

“Siwezi kusema usiende ikiwa tayari umesha panga hili jambo, ila nilicho hitaji kkushauri ni kuangalia ni jinsi gani ya utakavyo hangaikia na hiyo hali yako ya ujauzioto”

“Rani, natambua kwamba una wasiwasi mwingi juu yangu, ila usiwe na shaka, najua Mungu yu pamoja nami atanilinda leo, kesho na hata mimilele. Unajua nini mdogo wangu”

“Eheee?”

“Kwenye maisha yangu nimepitia mambo mengi sana, nimepitia mihangaiko mingi sana, hatukuzaliwa matajiri na Judy, tulikuwa ni masikini, tena masikini wale wa kuishi ushihilini kwenye chumba kimoja na mrehemu mama yetu. Miguu ya kuku na ugali ndii ulitukuza sisi, so sihofii kufa, labda cha kuhofia ni mtoto, ikiwa Mungu anajua ni nini ambacho ninakwenda kukifanya basi wala usiwe na shaka katika hilo”

“Sawa, mimi nilikushauri tu”

“Naelewa hilo wala usijali”

Judy akarudi huku akiwa na tabasamu.

“Umempata”

“Yaa nimempata nimeichukua namba yake na yeye ndio aliye nileta hadi hapo getini”

“Kwani ulienda kwa miguu?”

“Ndio”

“Walinzi wewe hawakusubui?”

“Ahaa….mimi wala sio star, wewe ndio star. Andika namba yake”

Judy akaanza kunitajia namba ya Jofu, nilipo maliza kuinakili katika simu yangu nikampigia. Simu yake ikaita baada ya muda kisha ikapokelewa.

“Haloo”

“Jofu niambie”

“Safi tu”

“Nani?”

“Ahaaa Jojo, niambie mchizi wangu”

“Safi aisee”

“Naona mdogo wako ana bastola za ukweli aisee”

“Hembu acha mambo hayo, kuna ishu nahitaji tuzungumze”

“Niambie tajiri wangu, naona siku hizi walinzi kede kede yaani bonge la superstar”

“Jofu hembu nisikilize kwanza hayo ya walinzi sijui usuperstar tuachane nayo kwa muda huu”

“Haya zungumza tajiri”

“Nahiyaji majira ya saa nane kamili usiku uje kunichukua hapa nyumbani na unipeleke uwanja wa ndege”

“Hee kwema?”

“Ndio kwema, vipi kwani?”

“Hamna kwa maana huo muda kwa mtoto mzuri kama wewe ni shida ikiwa una walinzi nini”

“Unahitaji dili au uhitaji?”

“Nahitaji mama?”

“Basi saa nane kamili nakuhitaji maeneo ya hapa nyumbani, utasimama nyumba mbili kuyoka hapa kwangu sawa”

“Sawa”

“Poa mida”

Nikakata simu na kuirusha kitandani. Nikachagua nguo chache za kuvaa pamoja na koti moja kubwa kiasi, nikaviandaa kabisa kwa safari. Muda ukazidi kuwenda, kadri jinsi muda unavyo kwenda ndivyo jisni wasiwasi na mashaka unazidi kuongezeka, kila muda nina jifikiria ni jinsi gani ninaweza kutoka humu ndani. Judy akachukua gari na kumsindikiza Rani kwao. Nikatoka chumbani kwangu na kushuka chini, nikatoka nje na kuwakuta walinzi wakiendelea kuimarisha ulinzi.

“Unatoka mdam?”

Mlinzi mmoja wa kiume aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.

“Hapana nahitaji kufanya mazoezi ya kunyoosha miguu”

“Sawa”

Nikaanza kuzunguka zunguka katika eneo la ndani ya jumba hili huku leo nikiwa makini sana kuichunguza sana kwa maana nahitaji kufahamu ni eneo ganin inaweza kulitumia katika kutoroka eneo hili. Kila eneo ambalo nina litazama kusema kweli halina dalili yoyote ya nipa upento wa mimi kutoka humu ndani. Na ubaya ni kwamba kumefungwa kamera za ulinzi kwenue kila upande wa uta nne za fenzi hii iliyo zunguka jumba hili.

‘Ehee Mungu nisaidie’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikiendelea kuzunguka eneo hili la hii nyumba. Hadi inatimu saa mbili usiku, sijajua ni jinsi gani nitatoka na mama mkwe tayari alisha fika hapa nyumbani, nikasalimiana naye na sote tukuingia ndani.

“Mumepika?”

“Hapana, Judy ametoka na yule rafiki yake”

“Ahaa, unajisikia kula nini mwanangu?”

“Chochote mama”

“Judy ametoka muda mrefu?”

“Yaaa nahisi foleni ndio inamchelewesha”

“Basi mpigie simu muambie aje na chakula”

“Chakula gani?”

“Chochote ukipendacho, naona kichwa kininiuma”

“Pole mama si unywe dawa?”

“Nimekunywa huko nitokapo”

“Chakula je?”

“Agizieni tu cha kwenu mimi nipo vizuri”

“Sawa mama, pole lakini”

“Asante”

Mama mkwe akapndisha gorofani na kuniacha sebleni, nikachukua simu yangu niliyo iweka kwenye mfuko wad era hili nililo livaa, nikaitafuta namba ya Judy na kumpogia.

“Upo wapi?”

“Nipo hapa Mwenge, kuna ajali imetokea basi ni foleni kubwa kama nini”

“Ajali ya nini?”

“Kuna bodaboda kagongwa na gari ndogo ndio polisi wanapima pima hapa”

“Nunua chakula uje nacho home”

“Chakula gani?”

“Chips mayai na kuku”

“Na cha mama?”

“Mama amesha kula”

“Poa”

Nikakata simu. Masaa yakazidi kusonga mbele majiri ya saa nne usiku Judy akarudi akiwa na chakula, kwa pamoja tukaanza kupata chakula hichi cha usiku. Masaa yakazidi kusonga kwa kasi sana, hadi inatimia saa sana na dakika arobaini usiku walinzi bado wanaendelea kuzunguka zunguka zunguka nje ya nyumba.

“Judy tunafanyaje?”

Nilizungumza kwa sauti ya chini huku nikimalizia kuvaa baibui jeusi, miwani kubwa kiasi na mtandio ulio zunguka vizuri kichwa changu na kuificha sura yangu kwa namna fulani.

“Nina wazo”

“Wazo gani?”

Judy akafungua mlango na kutoa ndani, gafla nikasikia kishindo kizito kwenye kordo na kujikuta nikikimbilia mlangoni, ila kabla sijaufungua mlango, nikahisika mlango wa chumba cha mama mkwe ukifunguliwa na nikajikuya nikishindwa kutoka nje, kwani mavazi haya niliyo yavaa naamini yatamuashiria mamamkwe kwamba nina sehemu ambayo ninahitaji kwenda na siri itabumburuka.



Kwa kasi yaa jabu nikavua nguo zangu nilizo zivaa na kuzitupia chini ya uvungu, hata kabagi kangu ka mngoni ambacho niliweka nguo kadhaa nacho nikasukumia mgongoni na kujilaza kitandani, kitendo cha kujifunika tu shuka, mama mkwe akaingia huku nikisikilizia mihemo yake ya nguvu na hatua zake, akanishika begani kwangu na kuanza kunitingisha taratibu.

“Jojo, Jojo”

Niliisikia vizuri sauti ya mama mkwe ila nikajifanya nimelala usingizi fofofo. Mama mkwe akaendelea kuniita kwa sauti ya chini ya upole kidogo.

“Mmmmm”

“Amka, mwenzioa amepata matatizo”

“Mmm…..”

Nilijifanya kuguna guna huku nikigeuka na kumtazama.

“Amka ukanisaisie Judy ameanguka”

“Ameanguka?”

Nijifanya kustuka huku nikikaa kitandani huku macho yakinitoka.

“Jikaze uje tumsaidie mwenzako huku”

Nikashuka kitandani huku nikiwa na nguo yangu ya ndani tu. Tukatoka nje ya chumba hichi na kumkuta Judy akirusha rusha miguu yake na mikono kama mtu mwenye kifafa. Hali hii ikaanza kunipa wasiwasi na mimi mwenyewe, nikajikuta nikipandwa na wasiwasi kwani sikuwahi kumuona Judy akiwa katika hali kama hii.

“Judy, Judy, Judy “

Niliita kwa sauti iliyo jaa mtetemesho mwingi sana. Mama mkwe akanyanyuka na kukimbilia nje nahsi amekwenda kuwaita walinzi waje kumsaidia.

“Acha uboya nenda kavae ujiande na safari”

Judy alizungumza huku akiwa akiyaweka macho yake sawa ambayo alikuwa ameyageuza kiasi cha kunifanya nichanganyikiwe.

“Pumbavu wewe”

“Nenda fasta mama anakuja, hii ndio nafasi ya pekee yak u……”

Judy haikuimalizia kauli yake mara tu baada ya kusikia hatua za watu zikipandisha kwennye gazi kwa haraka. Hata kabla sijanyanyuka nikamuona mama mkwe akiwa ameongozana na walinzi watatu wa kike.

“Mbebeni tumuwahishe hospitalini.”

“Sawa mkuu”

Walinzi hao wakamnyanyua Judy anaye endelea kurusha rusha miguu na kuanza kuelekea naye nje.

“Jojo utabaki hapa nyumbani sawa”

“Sawa mama”

Mama mkwe akaingia chumbani kwake, mara baada ya muuda akarudia akiwa amevaa trake suit pamoja na koti lake huku chini akiwa amevaa raba.

“Walinzi wachache watabaki hapa nyumbani sawa”

“Sawa mama”

“Nenda kapumzike”

Nikamshuhudia mama mkwe akikunja kona na kushuka kwenye ngazi za kuelekea chini. Nikiangia chumbani kwangu, cha kwanza kukifanya, nikakimbilia hadi katika dirisha ambalo linaelekea usawa wa dirisha langu linalo elekea usawa wa mbele wa jumba langu hili. Nikamuona wakimuingiza Judy ndani ya gari, geti likafunguliwa na gari mbili zikatoka ndani hapa kwa kasi sana. Idadi ya walinzi walio baki humu ndani ni wanne tu. Nikakaa kwa muda huku nikitafakari ni nini cha kutoka, kwani hii ndio nafasi yangu pekee kuhakikisha kwamba ninaondoka ndani ya jumba langu hili. Simu yangu ikaanza kuita kwa haraka nikaichukua na kuipokea.

“Oya vipi tena nimeona ndiga mbili zinatoka hapa kwenu spidi sana hadi nimeogopa mwanangu”

“Usihofu, nipe dakika kumi ninatoka”

“Kwema lakini?”

“Nimekuambia ni kwema, nipe dakika kumi ninatoka”

“Sawa dadake”

Nikakata simu na kuirushia kitandani. Nikalishika tumbo langu kwa muda kisha nikafungua kabati na kutoa mkanda maalumu ambao hutumika katika kupunguza ukubwa wa tumbo kwa wanawake wale wapenda kula kula sana. Nikaichukua na kuufunga vizuri tumboni na kuliziba tumbo langu vizuri. Nikachukua suruali yangu moja ya kitamba nyeusi, tisteti nyeusi, kisha nikachukua kitambaa ambacho ni cheusi na kujifunga nusu uso wangu. Nikachukua moja ya bushori kubwa jeusi na kulivaa kichwani mwangu. Nikasimama kwenye kioo, kwa jinsi nilivyo vaa ni ngumu sana kwa mtu kuweza kunitambua. Kwa haraka nikatoka chumbani kwangu hadi kwenye main switch. Nikazima umeme wa nyumba zima, nina imani ni jambo ambalo litawafanya walinzi kustuka sana. Kwa haraka nikatoka nje, giza kali limetanda eneo la nje. Kutokana nina uwezo mkubwa sana wa kupiga tana nikiwa na hisia kali za kuhisi ni wapi adui yangu alipo yeye kujua juu ya uwepo wangu ikaanza. Kila Mlinzi niliye kutana naye nikahakikisha kwamba nina mkwida kisawa sawa na kumzimisha kiasi cha kumfanya kwamba hato amka sasa wala baadaye. Jambo la kupigana na walinzi wa wane kwangu halikiwa gumu sana, kwani mimi mwenyewe nina jiweza kwa asilimia mia moja japo nilipo hakikisha walinzi wote wamepoteza fahamu,

Kwa haraka nikaingia ndani na kukimbilia gorofani, kwa haraka nikavu nguo zangu hizi na kuziweka kabatini, nikawasha taa ya simu yangu, iliyo pelekea chumba kizima kutawaliwa na mwanga mwingi, nikazitoa nguo zangu pamoja na kabegi kangu ka mgongoni ndani ya uvungu wa kitanda changu. Kwa haraaka nikaanza kuvaa, kama nilivyo kuwa nimevaa hapo awali. Nikatoka chumbani kwangu kwa mwendo wa kasi, nikashuka gorofani na moja kwa moja nikatoka kabisa nje uzio wa jumba hili, nikaelekea eneo ambalo nimemuelekeza Jufo anisubirie.

“Mbona unahema hivyo vipi?”

“Twende bwana”

Nilizungumza kwa msisitizo huku nikikaa vizuri kwenyepikipiki hii. Tukaondoka eneo la nyumbani hapa huku kwa mara kadhaa nikiwa ninatoa simu yangu na kuangalia muda.

“Ogeza mwendo”

“Aisee naisoma mia na ishiri mbona”

Jofo alizungumza kwa sauti ya juu kwa manaa kwa mwendo kasi wa hii pikipiki na upepeo mwingi ambao unatupiga kwenye nyuso zetu. Tukafanikiwa kufika katika uwanja wa ndege, huku ndege ambayo ninatakiwa kuondoka nayo ikiwa imebakisha dakika chache sana kabla haijaondoka, nikafungua begi langu mgongoni na kuchomoa noti kadhaa za dola ambazo sifahamu hata ni kiasi gani, nikamkabidhi Jofu na kuanza kukimbilia ndani. Nikapitia hatua zote ambazo ninatakiwa kuzipitia kama ambiria wengine, dada ambaye alitusaidia katika maandalizi ya safari hii akanipokea na moja kwa moja akanipeleka hadi kwenye ndege. Nikaitoa simu yangu mfukoni, nikatamani kumpigia Judy ila nikajikuta nikishindwa kabisa, kwa maana nina hisi kwambaa atakuwa yupo chini ya uanalizi wa madaktari pamoja na mama mkwe.Nikashusha pumzi taratbu kisha nikazima nikaizima simu yangu.

Taratibu ndege hii ikaanza kuondoka katika uwanja huu wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, ndani ya dakika kadhaa tukawa angani, nikafungua mkanda wangu huku nikishusha pumzi nyingi sana.

“Mbona una wasiwasi”

Mwanamama niliye kaa naye katika siti ya pembeni aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.

“Hapana”

Akshusha macho yake hadi kwenye tumbo langu, akatabasamu kidogo kisha akatingisha kichwa akionekana amejawa na furaha sana.

“Utazaa mtotoo mzuri wa kike”

Maneno ya mama huyu yakanishangaza sana na kujikuta nikimkazia macho.

“Samahani”

“Utazaa mtoto mzuri wa kike, mwenye afya njema na atakuwa ni mtu mkubwa sana kwa maisha yake ya hapo baadae”

Ikabidi nianze kumdadisi huyu mwana mama mwenye asili ya bara la Asia, vidole vyake vya mikono yake yote miwili amevaa pete nyingi zenye rangi ya kila aina.

“Usiogope, Jojo”

“Umelijuaje jina langu?”

“Ni rahisi kwa celebrate yoyote kuweza kufahamika”

Nikajikta nikitazamana na watu walipo siti za pembeni kuona kama wamenitambua kwa bahati nzuri nikawakuta wakiwa wanashuhulika na mambo yao na ni wazungu fulani.

“Kwa nini unahitaji kujipa hatari ambayo itakugarimu sana maisha yako”

“Una maanisha nini?”

“Utajua ni nini nina maanisha hapo mbeleni kwa sasa siwezi kukuambia”

“Kwanza wewe ni nani?”

“Hahahaa Jojo, unataka nikufahamu mimi ni nani?”

“Ndio”

Mama huyu akanichukua mkonono wangu wa kulia, akatazama kiganja changu, kisha akafumba macho huku usoni mwake alama za ndita zikanza kujichora taratibu. Akauuachia mkono wangu kwa haraka huku akihema jambo lilolo nishangaza.

“Kwa nini umeondoka Tanzania?”

Mama huyu alizungumza huku akiwa amenikazia macho yake.

“Ehee……?”

“Kwa nini umeondoka Tanzania?”

Nikapatwa na kigugumizi, nikatamani kumuhama mama huyu na kuamia siti hata nyingi ila kwa bahati mbaya siti daraja hili tulilopo zote zimejaa na nikihitaji kuhama daraja nilazima nifanye malipo mengine, ila kimoyo moyo nikaamua kujifariji nikisibiria kuona mwisho wake huyu mama.

“Hukupaswa kuwepo kwenye hii ndege kwa sasa hivi”

“Kwa nini unazungumza hivi?”

“Hii safari hii haito kuwa salama kwako”

“Kwa nini?”

“Naona hali ya hatari kubwa sana mbele yako, ni bora hata tukifika Kenya ushukr na urudi Tanzania”

Nikamtazama mama huyu nikaona ananifanya michezo ya kuigiza, moyoni mwangu tayari nimesha dhamiria kuhakikisha kwamba ninakwenda kumtafuta mume wangu popote kule alipo.

“Sikia mama, hunijui na wala wewe sikujui, sipendi uhuni, unataka kuniambia kwamba wewe ni msoma nyota au. Kama unaona hatari mbele ni bora kukumbana na hiyo hatari kuliko kufwata kile unacho niambia”

“Jojo kweli hutakiwa kuwa katika hii ndege, ni bora tukifika Jomo Kenyeta ushuke na safari yako iishie hapo”

“Unajua ni wapi ninapo kwenda?”

“Ndio ninafahamu, unapo kwenda. Unakwenda Russia, Mossow. Unakwenda kumtafuta mwanaume aliye kubebesha huo ujauzito ila ni vyema kuiahirisha safari hiyo”

Maneno ya huyu mama kidogo yakaanza kunistua, mapigo yangu ya moyo yakaanza kunienda kasi kidogo.

“Jojo hutakiwa kuwa katika hii ndege, tafadhali fwata kile nilicho kuambia, la sivyo utamkosa hata huyo ambaye unakwenda kumfwata kwa maana na yeye yupo kwenye wakati mgumu sana”

“Yupo kwenye wakati mgumu?”

“Niamabie mume wangu yupo kwenye wakati gani?”

Mama huyu akafumba macho yake, huku akinitazama, nikaanza kumuona macho yake yakianza kumwagikwa na mchozi, kwa wanja mwingi alio jiokoleza katika maeneo ya kulizunguka jicho lake yakasababisha machozi yake kuwa meusi.

“Niambie ni kitu gani ambacho kinaendelea kwa mume wangu”

“Usalama wako ni kushuka kwenye hii ndege”

“Eheee?”

“Ndio, ukitaka mume wako aendelee kuwa salama ni bora ushuke kwenye hii ndege”

Nikajikuta nikitetemeka sana, nguvu na hamu ya kuelekea nchini Russia ikaniishia kabisa, nikajikuta nikimtazama mama huyu. Sauti ya kike ikasikika ikituomba tufunge mikanda yetu, kwani tunakaribia kufika katika kiwanja cha ndege cha Jomo Kenyata nchini Kenya. Nikafunga mkanda wangu huku nikiendelea kumtazama mama huyu, taratibu ndege ikaanza kutua katika uwanja huu. Hadi ilipo tulia na milango kufunguliwa mwanama huyu akafumbua macho yake na kunitazama.

“Jojo shuka sasa”

“Nitashukaje iki…..”

“JOJO SHUKAAAAAA”

Mama huyu alizungumza kwa msisitizo hadi wazungu tulio kaa nao karibu wakanitazama. Taratibu nikafungua mkanda wangu wa siti, nikachukua kibegi changu cha mgongoni, nikaanza kuelekea kwenye mlango wa kushukia huku nikiwa nimejawa na huzuni kubwa sana.

“Mbona unashuka?”

Rafiki wa Judy aliniuliza huku akiwa amenishika bega. Nikamtazama kwa muda huku macho yangu yakiwa yamejawa na majonzi kiasi.

“Jojo niambie una nini?”

“Ninajihisi kuumwa, naomba nikapate matibabu nitaendelea na safari kuanzia hapa Kenya”

“Ni nini kinacho kusumbua sana?”

“Najisikia tu vibaya, kichwa changu kikinisumbua huwa kuna dawa ninatakiwa kutumia sasa sijazibeba”

“Tatizo ni hilo tu au kuna kingine hujakipenda kwenye safari hii yetu?”

“Hapana huduma zenu zipo vizuri tu”

Nilizungumza huku machozi yakinichuruzika usoni mwangu, nikageuka nyuma na kumtazama mama niliye kuwa nimekaa naye kwenye siti moja, akanikonyeza kwa macho yaliyo jaa machozi, akiniomba niendelee kushuka kwenye hii ndege.

“Safari njema”

Baada ya kumuambia dada huyu, nikaanza kupishana na watu wanao ingia ndani ya ndege hii, nikashuka na kuanza kutembea hadi eneo kuna basi maalumu ambalo hubeba abiria. Nikatoa simu yangu mfukoni, na kuiwasha, nikaingia ndani ya basi hili huku machozi yakinimwagika. Nikaka kwneye moja ya siti huku nikishuhudia mlango wa ndege hii ukifungwa, kisha taratibu ikaanza kuzunguka na kukaa sawa, ikaanza kwenda kasi katika run way, zake. Taratibu ikaanza kupaa angani, jambo lililo nifanya nijisikie vibaya sana kwani kwani shauku na hamu ya kusafiri kwenye nchini Russia imeishia nchi hii ya jirani na Tanzania ambayo ni Kenye. Gafla nikiwa katika kujilaumu, nikashuhudia mlipuko mkubwa sana kutoka katika ndege niliyo ipanda ambao ukapelekea hadi vioo vya gari hili kupasuka pasuka na kuturukia baadhi wa watu tuliomo ndani ni basi jambo lililo niogopesha sana na kujikiuta nikiishiwa na nguvu kabisa hadi nikajikuta nikiangusha simu yangu chini.



Ving’ora vya gari za zima moto zikaanza kukatiza kwa kasi kuelekea katika eneo ambalo vipande pande vya ndege hiyo vinaangukia. Taratibu nikaiokoa simu yangu, kisha nikasimama na kuanza kutembea kwa hatua za kujiburuza huku machozi yakiendelea kunimwagika usoni mwangu. Kitendo cha kukanyaga tu ardhi, nikajikuta nikianguka na kukaa chini pasipo hata kuyatajia. Heka heka ambazo zinaendelea katika uwanja huu wa ndege ambao hapo awali ulikuwa umetulia kidogo, kusema kweli kila kitu ninakiona kama ni ndoto au filamu.

“Hapana naota”

Nilizungumza mimi mwenyewe huku nikijifinya mkononi mwangu nione kama ni ndoto, ila si ndoto na ninacho kiona hapa ndicho kitu kinacho endelea kwa kweli. Nikastukia nikinyanyuliwa na kupakizwa kwenye kitanda cha matairi na kikaanza kusukumwa, kitu ambacho sikuhitaji hata kukiachia ni simu yangu pamoja na kiasi kabegi kangu ambacho nimekavaa bega moja. Nikaingizwa kwenye gari la wagonjwa na kuondolewa katika uwanja huu. Nesi na daktari waliomo ndani ya hili gari wakanitundukia dripu la maji, huku safari ikizidi kuendelea.

Tukafika hospitalini na moja kwa moja nikapelekwa katika chumba cha matibabu, nikaanza kukaguliwa mwili wangu, pasipo kujijua kumbe nina jeraha kubwa kwenye eneo la mbavu upande wa kushoto. Damu nyingi sana kumbe zimenitoka, kitu ambacho kusema kweli kwa hapo awali sikuweza kufahamu chochote.

“Dokta”

Niliita kwa sauti ya upole huku nikimtazama daktari huyu anaye nishona jeraha langu.

“Naam”

“Kidonda ni kikubwa sana?”

“Hapana kioo kimekuchana ila hakijaingia ndani sana”

“Ahaa….kwa hiyo kinaweza kuathiri mtoto wangu?”

“Hapana hakiwezi kabisa kumuathiri mtoto na mimba yako ipo salama”

“Hiyo damu munayo niwekea ipo salama”

“Asilimia mia moja, tumeipima na kuhakikisha kwamba haina maradhi wala virusi vya HIV”

“Sawa dokta”

Daktara huyu kusema kweli ni mkarimu na maswali yangu amejayajibu kwa ukarimu sana ambao ni tofauti kidogo na madaktari wengine hususani kwa nchi yetu ya Tanzania huwa baadhi yao wanakuwa na dharua na majibu ya mkato mkato.

“Hivi kwenye ile ndege kule wamepona?”

“Hadi sasa hivi sijafahamu ripoti maalumu”

“Sawa”

Baaada ya dakika kama kumi na mbili hivi daktari akanimaliza kunishona eneo hili la mbavu zangu, nikatolewa katika chumba hichi na kuingizwa katika chumba cha kwangu peke yangu ambacho kina kitanda kimoja, sofa wanalo weza kukaa watu wawili, meza ndogo ya kioo na tv.

“Je ninaweza kuwasiliana na Tanzania?”

Daktari huyu alizungumza na kunifanya nistuke kidogo.

“Kivipi?”

“Jojo unajulikana sana, kwa kama utahitaji niweze kufanya mawasiliano na watu wako walipo nchini Tanzania tunaweza kuwasiliana”

“Hapana”

Daktaria kanitazama kwa muda kisha akatingisha kichwa akimaanisha kwamba kile nilicho mueleza amekielewa vizuri.

“Nitakuwa ninakupatia uangalizi mzuri na wakaribu sana”

“Nashukuru sana”

“Ninaitwa Dokta Calvin”

“Nashukuru dokta Calivin, ninaomba simu pamoja na lile begi langu”

“Sawa”

Dokta Calvin akatoka ndani humu na baada ya muda kidogo akarudi akiwa na vitu vyangu nilivyo mugiza, nikafungua begi langu na kukuta hakuna kitu kilicho pungua. Dokta Calivn akaniaga akidai kwamba anakwenda kushushulika na wagonjwa wengine. Nikatamani kuwasha simu yangu kwa muda huu ila nikasita kidogo kwani ni majira ya saa kumi na moja alfajiri. Nikawasha vt na kuendelea kutazama katika chanel ya Citizen, ambao wanaonyesha hali halisi ya kila kitu kinacho endelea katika uwanja wa ndege.

Sura ya yule mama aliye niasa kwamba nishuke kwenye ndege, ikaanza kunijia kichwani mwangu, sauti yake nikahisi kama bado ninaisikia masikioni mwangu. Hadi inafika saa moja na nusu asubuhi, ndipo waziri anaye shuhulika na maswala ya anga katika nchi hii ya Kenya akatoa ripoti inayo sema kwamba watu wote ambao walikiwa kaika ndege hiyo wamefariki dunia, kitu ambacho ninatambua fika, endapo Judy ataiona habari hiyo ni lazima atachanganyikiwa, kwa maana yeye mwenyewe ndio anaye fahamu juu ya safari yangu hii.

Nikawasha simu, kwa bahati mbaya mtandao ninao utumia kwa nchi hii ya Kenya hautumiki, nikiwa katika harakati za kujaribu nijue nini natakiwa nifanye. Dokta Calvin akaingia ndani humu.

“Unaendeleaje?”

“Kwa mbali nahisi maumivu”

“Hapo inabidi nikuchome sindano ya kupunguza maumivu, na ndripu hilo likiisha hatataongeza dripi jengine”

“Sawa dokta”

Dokta Calvin akanitazama kidonda changu kwa sekunde kadhaa, kisha akanichoma sindano ya kupunguza maumivu.

“Dokta ninaweza kupanda line ya hapa Kenya”

“Ndio”

“Naomba unisaidie katika hilo”

Nilizungumza huku nikitoa noti ya dola mia moja, nikamkabidhi daktari huyu.

“Mbona umenipatia kiasi kikubwa hivi?”

“Nahitaji hicho kiasi uweze kukitumia katika kuninunulia na chakula pia, kikiisha basi utanijulisha niweze kukupatia kiasi kingine ila kwa sasa naomba unipatatie hiyo laini na uniwekee vocha ya kutosha”

“Sawa”

Dokta Calvin akatoka ndani humu. Baada ya muda kidogo, akaingia daktari mwengine huku akiwa ameongozana na wanaume wawili walio valia suti nyeusi.

“Habari yako”

“Salama”

“Mimi naitwa dokta Moli, ni daktari mkuu wa hii hospitali hapa, na hawani ni wana usalama wametoka makao maku ya serikali, kuna maswali wanahitaji kukuhoji tungependa uwape ushirikiano.”

“Sawa”

“Ninaitwa detective Onyango, na mwenzangu anaitwa detevtive Othuman”

“Nashukuru kuwafahamu”

Detective Onyango akafungua laptop yake na kuiwasha. Akaweka picha za video za abiria wote walio kuwa kwenye ndege hiyo ikiwemo mimi mwenyewe.

“Hii ni list ya abiria ambao walikuwa ndani ya hii ndege, ikiwemo wewe mwenyewe. Safari ilianzia nchini Tanzania hadi kufika hapa nchini Kenya, na ratiba inaonyesha kwamba ilitakiwa kufika hapa nchini Kenya muda wa saa kumi na nusu, na kweli ilifika muda huo”

“Sawa”

Niliitikia huku nikitingisha kichwa na kuwatazama wapelelezi hawa.

“Wewe safari yako haikutakiwa kuishia nchini Kenya, na ilitakiwa kuendelea hadi nchini Russia, ila inavyo onyesha wewe peke yako ndio ulishukia nchini Kenya, na baada ya muda mchache ndege ikalipuka, je ulikuwa unafahamu kwamba kuna mlipuko ambao unakwenda kutoka?”

“Hapana”

“Kwa nini hapana ikiwa ndege mara tu ya kupaa angani katika muda mchache ililipuka?”

“Mimi sikufahamu kama ndege inakwenda kulipuka, mimi nilishuka baada ya mtu niliye kaa naye kwenye siti moja kuniambia niweze kushuka.”

“Haiingii akilini mtu akuambie ushuke na wewe ukashuka kama si bomu ambalo umelitege ndani ya ndege na kupelekea ndege kulipuka”

“Samahani, unasema bomu?”

“Ndio umeweka bomu ndani ya ndege na ndio sababu ya ndege hiyo kulipuka?”

Mlango ukafungulia na akaingia dokta Calvin huku akiwa ameshika mfuko mweusi ambao unaonyesha kwamba una chakula ndani yake.

“Samahani dokta tunamazungumzo na mgonjwa wako, tunakuomba utupishe kwa sasa”

Ditective Othumani alizungumza huku akimtazama dokta Calvina.

“Samahani”

Dokta Calvin alizungumza na kutoka chumbani humu. Ditective Othumani akanigeukia na kunitazama usoni mwangu, huku uso wake ukiwa umejaa makunyanzi yanayo ashiria ana hasira na uchungu dhidi yangu.

“Ngoja niwaambie kitu kimoja, mimi sio gaidi, na wala sihusiki katika huo mlipuko wa bomu”

“Unahusika”

Nikafumba macho huku hasira ikianza kunipanda taratibu kwani kwenye maisha yangu kitu ambacho sikipendi ni kusingiziwa jambo ambalo sijawahi kulifanya kabisa kwenye maisha yangu.

“Na kupitia hili basi adhabu yako ni kifo”

“Hahaaa…..sikiani nyinyi, sijafanya kosa la aina yoyote, pili safari ya mimi kuelekea Russia na kuikatisha ni maamuzi yangu mimi kama abiri na kama kuna ushahidi ambao unaonyesha kwamba nimeweka bomu ndani ya ndege ile ninaomba munionyeshe”

“Ushahidi utakwenda kutolewa mahakamani”

“Sawa, ila niwashauri kitu kimoja, rudini tena kwenye mafunzo yenu ya upelelezi na musifanye kazi kwa hasira na mufanye kazi yenu kwa umakini. Video hapo inawasuta na kuwaonyesha kabisa kwamba nimeingia kwenye ndege, nimekaaa na nikashuka, sikunyanyuka hata kwenda chooni, kama ni bomu nimeliweka vipi, na limekaaje. Musipende kumbambikia mtu kesi za kipuuzi baada ya kufahamu kwamba anaweza kuwapatia chochote kitu, sipendi ujinga na mukumbuke mimi sio Mkenya ni mtanzania na ni mtu maarufu sana ndani na nje ya nchi yangu, sasa kama munahitaji kazi ya ulinzi katika kampuni yangu nitawapatia sawa”

Nilizungumza kwa hasira huku machozi yakinimwagika usoni mwangu. Wapelelezi hawa wakatazamana huku wakionekana kuishiwa pozi. Onyango akaifunga laptop yake.

“Tutarudi tena kukuhoji maswali?”

“Mukija tena hakuna swali nitakalo wajibu ikiwa hamuna ushahidi wa mimi kuweza kuhusika katika ajali, kwanza niwaulize kitu imekuwaje munihisi mimi, badala ya kuniuliza ilikuwaje kuwaje munaniambia nimeweka bomu acheni ujinga”

“Jamani mgonjwa atakuwa katika hali mbaya naomba muweze kutoka”

Daktari huyu alizungumza kwa msisitizo. Wapelelezi hawa wakanitazama kwa muda kisha wakatoka chumbani humu.

“Unajisikiaje?”

Daktari aliniuliza kwa sauti ya upole

“Salama, ila sihitaji hao watu waingie tena chumbani kwangu”

“Sawa”

Daktari akatoka, dokta Calvin akaingia na moja kwa moja akanifwata hadi kitandani huku akionekana kujawa na wasiwasi mwingi sana.

“Walikuwa anahitaji nini?”

“Eti wananihoji kuhusina na mlipuko wa ndege na wanasema kwamba mimi nimehusika”

“Umehusika, kivipi?”

“Eti nimeweka bomu kwenye ndege hiyo”

“Khaa, kama ungekuwa umeweka bomu leo hii ungekuwapo hapa hospitalini si ungekuwa umesha toroka?”

“Wewe daktari tu una upeo huo na kulijua hili, ila hao wapelelezi ni wapuuzi sana.”

Nilizungumza huku nikifuta machozi yangu usoni.

“Nimefanikiwa kupata line, nimesha iweka vocha ya kutosha na pia nimekuchukulia chuakula, chips na mayai sijajua unapenda?”

“Yaa japo ni asubuhi ila nitakula hivyo hivyo”

Nikaichukua simu yangu na kutoa laini ya mtandao wa Tigo kisna nikaiweka line hii ya mtandao wa Safaricom. Nikaitafuta namba ya Judy na kuanza kumpigia, simu yake ikaanza kuita, ila baada ya muda kidogo ikakata. Nikarudi kuipiga kwa mara zaidi ya sita ila hajapokea kabisa.

“Vipi?”

“Ninampigia mdogo wangu ila hapokei simu”

“Labda yupo mbali na simu au amelala kwa maana si unajua hii ni asubuhi”

Sikumjibu dokta Calvin chochote, nikaitafuta namba ya mama mkwe kwenye orodha ya majina ya watu walipo katika simu yangu na nikafanikiwa kuweza kuipata. Nikashusha pumzi nyingi sana huku nikiitazama namba hii kwa maana nina tamani kumpigia na kumueleza eneo nilipo na matatizo ambayo tayari yamesha jitokeza na mengine yanaanza kujitokeza, ikiwemo la wana usalama kunihisi nimehusika kwenye ajali ya kulipuka kwa ndege hiyo. Ila tukio la kuwapiga walinzi katika jumba langu ambao wameweka na mama yangu mkwe, nilipo likumbuka tu kichwani mwangu mikono yangu ikaanza kutetemeka na hata hamu ya kuwasilana na mama yangu mkwe ikanipotea kabisa.



“Vipi?”

Dokta Calvin aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu, ila sikuweza kumjibu kitu cha aina yoyote zaidi ya kukaa kimya nikiitazama simu yangu. Nikajitahidi kushusha pumzi nyingi sana ili kuondoa wasiwasi wangu nilio nao. Nikamkumbuka wifi yangu, nikaitafuta namba yake na kumpigia simu. Simu yake ikaanza kuita kwa muda kisha ikapokelewa.

“Halooo”

Niliisikia sauti ya wifi nikaa kimya kwa muda huku nikiemsikilizia wifi jinsi anavyo zungumza haloo haloo.

“Mmmmm mtu mwenyewe hazungumzi”

‘Ni ni nani?’

Niliisikia sauti ya mama mkwe kwa mbali, ikionyesha kwmaba muda huu wifi yupo karibu na mama.

“Hata sijui na namba yenyewe wala sio ya Tanzania”

“Hembu niione”

Nikakata simu bila kupenda na nikaizima kabisa, kwani sasa hivi ninajikuta ninamuogopa sana mama yangu mkwe, kwani kitu nilicho weza kukifanya kwa walinzi wake kusema kweli sijui hata nifanye kitu gani.

“Docta Calvin”

Nilitwa kwa sauti ya upope huku nikimtazama dokta Calvin aliye shika simu yake akionekana kama anamjibu mtu meseji.

“Naam”

“Ahaa….a…basi”

“Basi, ulihitaji kuniambia nini Jojo”

“Hapana usijali”

“No. Zungumza tu kuwa huru na mimi wala usijali”

“Hapana”

“Au ulikuwa unahitaji kuhusiana na hawa wapelelezi walio kuja kukusumbua hapa?”

“Hapana, tutazungumza baadae kwa sasa ninaomba nipumzike”

“Sawa Jojo hakuna matata”

“Okay”

Dokta Calvin akatembea hadi mlango kisha akasismama kwa muda huku akionekana kuzingatia sana mtu ambaye anachati naye.

“Unachati na girl friend wako nini?”

“Hahaahaa….yaaa jua hawa mademo wa hapa Kenya wengi wamejaa matata. Manzi nimempa elfu kumi eti sasa hivi anataka tena nimpe akafanye shoping”

“Hahaa elfu kumi ya hapa kwenu au ya Tanzania”

“Ya hapa kwetu”

“Ahaaa, mpatie nyingie bwana”

“Pesa nitoleee wapi Jojo, shahara zenyewe hazijapanda serikali bado inatusaua”

“Poleni sana”

“Asante”

Mlango ukafunguliwa, wakaingia madaktari wawili walio funika nyuso zao kwa vitambaa. Dokta Calvin kwa ishara ya mkono akawaonyooshea madaktari hawa sehemu nilipo lalala mimi.

“Dokta, ni nini kinacho endelea?”

“Samahani sana jojo”

Kabla hata sijanyanyuka madaktari hawa wakaniwahi kwa kunibana mikono yangu na kunikatamiza kitandani kwa nguvu sana.

“Haloo Jojo”

Sauti ya Nuru iliyo toka kwa daktari mmoja anaye onyesha ni mwaamke ilinistua sana, akakishusha kidogo kitambaa chake, hapo ndipo nikadhihirisha kwamba huyu aliye nikamata hapa ni Nuru. Nikajaribu kufurukukata ila kwa haraka wakanichoma sindano ya shingoni na kusukuma dawa yote iliyo kuwemo kwenye bomba la sindano hiyo. Mawenge mawenge yalioyo ambayana na ukungu yakaanza kunitawala macho yangu na baada ya dakika kama moja nikajikuta nikilala usingizi fofofo.

***

Upepo mzuri ukaanza kupenya kwenye ngozi yangu. Ukimya ulipo ndani humu ukanifanya nifumbeu macho yangu. Nikaanza kutazama kila eneo sehemu ya chumba hichi kilicho pakwa rangi nyeupe na kila kitu kilichopo humu ndani ni rangi nyeupe. Ubaya wa hichi chumba hakina kabisa dirisha wala mlango wake sijui unaonekana kwa wapi. Nikaka kitako na kujitazama mwilini mwangu, vazi nililo livaa hapa ni jeupe, kwa haraka nikashuka kitandani huku nikichomoa mrija wa dripu hili la maji nililo chomwa kwenye mkono wangu wa kushoto. Nikaanza kutazama kila eneo la chumba hichi hili niweze kuona ni wapi nilipo ila ninashindwa kufahamu kabisa.

“Haloooo”

Nilijikuta nikita kwa nguvu, kitendo kilicho nifanya nihisi maumivu makali kwenye upande wangu wa mbavu ambapo niliumia.

‘Ehhee Mungu nipo wapi jamani’

Niliendelea kuzungumza kimoyo moyo, kwani kwenye maisha yangu sijawahi kuingia katika sehemu kama hii.

‘Heii’

Nilijitahidi kuita ila nikahisi kama sisikiki kwa maana kama tu mlango wenyewe siuoni basi ni sehemu ambayo siwezi kusika na mtu yoyote.

‘Nuru’

Nilimuwaza Nuru kichwani na kujikuta nikirudi kitandani huku nikihema sana na wasiwasi mwingi ukiwa umenitawala.

‘Nuru ndio ameniteka, mshenzi huyu safari hii nitamuua mimi mwenyewe’

Nikiwa katika dimbwi la mawazo hayo, kimlio kidogo cha kengele kikalia, moja ya sehemu ambayo kwa kuitazama utaona ni ukuta usio na dalili yoyote ya mlango, ikafunguka. Akaingia Nuru akiwa amevalia mavazi meupe huku tabasamu pana likiwa limejaa usoni mwake.

“Wewe mshenzi, mbwaaa weweee…..”

Nikajaribu kumsogelea Nuru kwa hasira, ila maumivu makali niliyo yahisi kwenye mbavu zangu yakanifanya nishindwe kabisa kufanya chochote.

“Utajiumiza bure, tulia unisikilize habari nzuri sana ambayo ninahitaji kukuambia”

“Nuru nitakuua, nitakuua Nuru, wewe endelea kunisumbua tu”

“Eti ehee?”

“Ndio wewe endelea kunisumbua tu”

“Sawa, nimekuja kukuweka hapa hadi utakapo pona, kisha baada ya hapo tutaendelea kuwa pamoja mimi na wewe”

“Hahaaa…..hivi hujaona wanawake wengine wakusagana nao hadi uje unichukue mimi?”

Ndio sijawaona ndiomaana nina hangaika usiku na mchana kuhakikisha kwamba ninakurudisha mikononi mwangu. Jojo tambua kwamba nina kupenda na nina kuhitaji kwenye maisha yangu kwa nini hutaki kunielewa eehee”

Nuru alizungumza huku akinikalisha kitandani taratibu.

“Natambua kwamba una hasira kali sana na mimi, ila sijafanya kitu chochote kibaya kwako na nimekaa na kujifikiria kwamba endapo nitakufanyia wewe kitu kibaya kwako basi huto nipenda tena. Tafadhali Jojo nakuomba utulie nami, nakupenda sana”

Nuru alizungumza kwa sauti ya upole na iliyo jaa hisia kali za kimapenzi. Nikaka kimya kwa muda huku amkono wake wa kulia akinishika shika juu ya mapaja yangu.

“Jojo, makosa yote ambayo umenifanyia nimekusamehe mpenzi wangu, sinto fanya tena fujo juu yako na watu wa karibu yako, kikubwa ninakuomba uweze kunipenda”

“Unahisi pesa zinaweza kunua upendo, unahisi pesa zinaweza kununua maisha ya mtu eheee?”

Nilizungumza kwa uchungu mwingi sana huku machozi yakianza kunilenga lenga usoni mwangu.

“Natambua kwamba hayawezi kufanya hicho kitu”

“Sasa jee?”

“Ila Jojo elewa, nimejaribu kutumia nguvu nikihisi kwamba utanipenda, ila hujaonyesha hata theluthi ya upendo wako kwangu”

Nuru naye machozi yalianza kumwagika usoni mwake.

“Nakuhitaji Jojo, wewe basi nidanganye tu kama una nipenda, nidanganye tu upo tayari kuwa na mimi nami nitafurahi kwa maana moyo wangu una maumivu makali ila huhitaji kuyasikia wala kuyapenda”

Nuru aliendelea kuzungumza huku akinishikwa shingo yangu, taratibu akaanza kunisogezea uso wake, nikatulia kimya huku machozi nami yakiendelea kunibubujika katika mashavu yangu. Alipo zifikisha lipsi zake mita chache sana nikaviweka vidole vyangu viwili vya mkono wa kulia katika lipsi zake huku nikimzuia.

“Nipo wapi hapa”

“Eheee?”

“Umenisikia nipo wapi?”

“Tupo Dubai”

Nikashusha pumzi taratibu, kwani sehemu nilipo ni mbali sana na nchi yangu ya Tanzania.

“Kwa nini unapenda kuniweka mbali na familia yangu”

“Sio kama ninapenda, ila wewe ndio unasababisha iwe hivi, kwa nini usikuuhurumie moyo wangu, hembu tazama jinsi nilivyo kondo sasa hivi Jojo, yote ni kwa ajili ya mawazo yako wewe, kwa nini lakini ehee?”

Nuru alizungumza huku akisimama, akavua dera alilo livua, na kweli amepungua mwili wake, sio Nuru yule ambaye nilisha mzoea kumuona amenona mwili wake.

“Sina mtoto, sina ndugu sina chochote zaidi yako wewe, kwa nini lakini unataka kuniweka mbali Jojo ehee.”

Nuru akaka kitandani hapa, akauchukua mkono wangu wa kulia na kinishikisha katika kitumbua chake.

“Shika….shika uone jinsi kulivyo jaa joto. Nihurumie Jojo”

Nuru alizungumza huku akijaribu kuhakikisha kwamba anakiingiza kidole changu cha katikati katika kitumbua chake.

“Ila nina umwa”

Nilizungumza huku nikijiyahidi kutoa kidole changu kwenye kitumbua chake ambacho kusema kweli ni cha moti mithili ya mwanamke mwenye mjamzito kama mimi.

“Nakuomba Nuru, nina umwa, nakuomba nipate tu nafuu kisha tutakuwa tunafanya hivi hadi uchoke.”

“Umenikubali”

“Ndio nimekukubalia, ila nina sharti moja”

“Zungumza tu sharti lako”

“Ninakuomba umsaidie mume wangu kule alipo, naamini anahiyaji msaada wa kurudi nyumbani nchini Tanzania”

Nuru akaka kimya kwa muda huku akinitazama usoni mwangu, habari ya kumtaja mume wangu nina amini kwamba itakuwa imemkera kwa asilimia kubwa sana.

“Tafadhali nakuomba Nuru, kama unanipenda, msaidie mume wangu”

Nuru akasimama, taratibu akaokota dera lake na kulivaa mwilini mwake pasipo kunisemesha kitu chochote.

“Mwanaume uliye naye sio sahihi kwako kwenye maisha yako, sijaelewa ni kwa nini unaendelea kumng’ang’ania, kwa nini lakini Jojo?”

“Awe sahihi, asiwe sahihi ila nina mpenda, ndio maana nime amua kumbebea mimba yake”

“MIMBAAAA……!!!?”

Nuru alizungumza huku akinishangaa sana, uso wake ukajaa ndiza kadhaa, zinazo muashiria kwamba ana hasira kali iliyo tokana na habari hiyo niliyo mueleza. Nikamjibu kwa kutingisha kichwa nikumdhihirishia kwamba ni kweli mimi ni mjamzito.

“Huwezi kuwa na mimi, huku ukiwa umebeba mimba ya mwana haramu kama Eddy, ni lazima mimba hiyo itoke tene lao hii hiii”

Nuru baada ya kumaliza kuzugumza maneno hayo akaanza kutembea kuelekea katika eneo alilo ingilia jambo lililo nifanya mwili wangu mzima kunitetemeka kwa woga kwani sasa ninapaswa kupigania maisha ya mwanangu ajaye aliyopo tumboni la sivyo, nitamshuhudia akikatishiwa ukuaji wake ndani ya tumbo langu hili.



“Nuru”

Niliita kwa sauti ya upole huku nikimtazama Nuru aliye simama hatua chache kutoka ulipo mlango alio ingilia, taratibu akanigeukia na kunitazama usoni mwangu.

“Wewe ni mwanamke kama mimi, mwanamke ambaye unaweza kupaa maumivu kama mimi ukiona kitu kama hicho ulicho kidhamiria kukifanya”

Niluzungumza huku machozi yakinimwagika usoni mwangu.

“Kama unanipenda kweli, mpende na mwanangu. Mwanangu hana kosa lolote, mwanangu anahitaji kuionja hii pumzi ambayo ni ya bure tuliyo pewa na mwenyezi Mungu. Nakuomba usimfanyie hivyo mwanangu”

Niliendelea kuzugumza huku nikilia kwa uchungu sana, kwani hapa nilipo sina uwezo wa kupambana kujiokoa mwenyewe, silaha yangu kubwa kwa sasa ni maneno yangu ya ushawishi ambayo ninaweza kumuambia Nuru na kunielewa. Nikayaona machozi ya Nuru yakichuruzika kwenye mashavu yake.

“Nipo tayari kufanya kitu chochote utakacho kisema juu yangu, ila nakuomba Nuru nipo chini ya miguu yako”

Nilizungumza huku nikishuka kitandani nikapiga magoti chini. Kwa haraka Nuru akanifwata sehemua mbayo nipo na kunikumbatia kwa nguvu huku na yeye akiangua kulio kizito, kilicho nyanyua na mimi hisia zangu za kulia na kujikuta na mimi nikilia kwa nguvu. Tukakumbatia kwa dakika kama tano, kisha Nuru akaniachia, akanishika mashavuni mwangu kwa viganja vyake viwili, taratibu akanibusu mdomoni mwangu, sihitaji kumuudhi kwa lolote, hii yote ninafanya kwa ajili ya mwanangu kipenzi. Taratibu tukaanza kunyonyana midomo yetu.

“Jojo”

“Mmmmm…”

“Unaniahidi utafanya chochote nitakacho kihitaji?”

“Yaaa chochote ili mradi umuache mwanangu hai, mwanangu hana kosa lolote ambalo lina mpasa kutolewa kwa sasa”

“Nakuahidi kuto kumuua mwanao na nitamuheshimu sana mwanao. Ila kuna jambo moja ninahitaji kutoka kwako, ukilikataa hilo basi ahadi yangu itabaki na kuendelea kuwa pale pale.”

Nikaka kimya kwa muda huku nikimtazama Nuru usoni mwake.

“Jambo gani hilo?”

“Nahitajiti tufunge ndoa ya halali sasa”

Katika pigo na wazo ambalo sikuwahi kulitegemea wala kulitarahijia basi ni hili. Kwa upande mmoja kusema kweli sihitaji kabisa maswala haya ya usagaji yaendelee kwenye maisha yangu, ila kutokana na usalama wa mwanangu sina namna yoyote ya kufanya.

“Holoo mbona kimya”

“Hamna, naomba muda wa kufirikia juu ya hilo swala kama huto jali?”

“Sawa ninakupa muda wa kufikiria, mwanao au ndoa yetu”

Nuru baada ya kumaliza kuzugumza maneno hayoa akaondoka eneo hili na kuniacha nikiwa nimesongwa na mawazo mengi sana. Kila akili yangu inapo gota katika kumuwaza mume wangu Eddazaria ninajikuta moyo wangu ukiniuma sana na kuhisi kama kisu kikali kinakatika katika moyo wangu na kuurarua vipande vipande.

“Eddy upo wapi jamani mume wnagu”

Nilizungumza huku machozi yakinimwagika usoni mwangu. Masaa, siku na wiki zikapita, jeraha langu likapona kabisa, huku nikiendelea kupata huduma zote ndani ya chumba hichi. Nuru kadri kila iitwapo leo basi hunifanya mambo yaliyo meme kuhakikisha kwamba hujiweka karibu kabisa na mimi. Daktari maalumu aliye muweka kwa uangalizi wangu kila siku anahakikisha anaangalia makuzi ya mimba yangu kwa ukaribu wa hali ya juu sana.

“Dokta ninaweza kufahamu mwanangu ni wa jinsi gani?”

Nilimuuliza dokta Khan huku nikimtazama usoni mwake.

“Yaa unaweza kufahamu ila tusubiri kwa muda muda kidogo”

“Kama akiwa na miezi mingapi?”

“Mmmm…sita hizi kwenda mbele, hapo kidogo kuna kuwa na uhakika wa kuweza kufahamu jinsia halisi ya mtoto”

“Ahaaa, ila afya yake si njema?”

“Asilimia mia moja, na utazaa mtoto mwenye kilo nyingi sana”

“Mmmm si ataniumiza jamani”

“Yaaa ila kuna njia mbili za kuweza kujifungua. Njia ya kawaida na njia ya upasuaji, ukishindwa njia ya kawaida, itabidi tukufanyie upasuaji”

“Mmmmmm”

“Yaa usiogope”

Nuru akaingia chumbani humu akiwa amebeba mdoli mkubwa sana na mwenye rangi nyeupe. Akasalimiana na daktari kisha akasalimiana na mimi huku akinibusu mdomoni mwangu.

“Unajisikiaje mpenzi wangu?”

“Nipo poa, hili doli jamani mbona ni kubwa sana”

“Mmmm litakuwa linakulinda kipindi nikiwa sipo”

“Jamani”

“Yaaa, eheee dokta nipe ripoti ya mgonjwa wangu?”

“Anaendelea vizuri sana na hana tatizo lolote ambalo linaweza kumsumbua kwa sasa”

“Ohoo asante Mungu kwa maana kila siku nilikua ninamuomba Mungu aweze kunisaidia katika hili. Sasa ninaweza kumchuku sasa?”

“Yaa munaweza kutoka”

“Asante sana dokta Khan kwa msaada wako wote ulio weza kumsaidia mpenzi wangu”

“Nijukumu langu madam”

“Tunakwenda nyumbani sasa”

Nuru alizungumza huku akiwa amejawa na furaha kubwa sana. Sikuwa na usemi wowote zaidi ya kufurahi kwa kutabasamu japo akilini mwangu sasa ninaanza kupanga mipango mipya ya kuhakikisha kwamba ninatoka mikononi mwa Nuru hata kabla ya adhimio lake kukamilika. Dokta Khan akakusanya baadhi ya vifaa vyake ambavyo aliniweka hapa hospitalini, kwa ajili ya kunichunguza afya yake baada ya kumaliza hivyo akaviweka kwenye kibegi chake kidogo kisha akatoka chumbani humu na kutuacha na Nuru.

“Jojo, hivi unaikumbuka siku yako ya kuzaliwa?”

“Aha…aaaa yaa ni kesho”

“Nilijua labda umesahau, basi kesho nitahakikisha kwamba nakufanyia sherehe ambayo hujawahi kufanyiwa kwenye maisha yako”

“Asante”

Nilijibu kwa ufupi kidogo huku ni nikimtazama Nuru usoni huku kimoyo moyo nikisema kwamba hajui ni kitu gani ambacho ninapanga kumfanyia. Wakaingia wafanyakazi wanao msaidia Nuru baadhi ya wasichana wawili nina wafahamu kwa maana nilisha waona siku walivyo kuja hospitali jijini Tanga, Eddazaria alipokuwa amelazwa. Wakabeba mabegi yangu ya nguo kadhaa ambazo Nuru alikuwa akininunulia kila siku alivyo kuwa akija kunitazama.

“Nyumbai kwako ni wapi?”

“Utapaona tu mpenzi wangu wala usiwe na wasiwasi mwingi”

“Kweli?”

“Ndio, lazima nikuepeleke katika sehemu ambayo itakuwa ni salama kwa ajili yako”

Tukatoka chumbani hapa, tangu nilipo ingizwa nikiwa sijitambu leo ndio mara yangu ya kwanza kuyoka ndani humu. Hili ni jengo ambalo ni kubwa kubwa na lina ulinzi wa hali ya juu. Tukaingia kwenye lifti hapa ndipo nikagundua kwamba hili jengo lina gorofa zaidi ya mia nne themanini na gorofa hii tuliyopo ni gorofa namba mia nne.

“Mbona tunakwenda juu?”

Nilimuuliza Nuru mara baada ya kumuona ameminya batani ya goroa ya mwisho kabisa inayo tupeleka juu. Tukafika juu ya gorofa hii na kukuta helicopter mbili zikiwa zinatusubiria, tukaingia kwenye helicopter ya kwanza sisi wa wili huku wasaidizi wake wakiingia kwenye helicopter ya pili.

Taratibu Nuru akanishika tumbo langu ambalo kila jinsi siku zinavyo zidi kwenda ndiyo jinsi linavyo zidi kukua.

“Unajua hapo awali nilimchukia kiumbe uliye mbeba, ila kwa maneno ambayo siku ile ulivyo nieleza nilijikuta chuki yote ikiniondoka moyoni mwangu na kuanza kumpenda.

“Nashukuru kwa upando wako huo, ila nina swali ninaomba nikuulize”

“Uliza tu?”

“Umeweza kufwatilia taarifa yoyote kwa nchi ya Tanzania kuhusiana nami?”

Nuru akakaa kimya huku akinitazama mimi usoni mwangu.

“Tutazungumza huku tukifika nyumbani”

Jibu la Nuru kidogo likaanza kunipa mashaka, mapigo yangu ya moyo yakaanza kunienda kasi.

“Ona kule?”

Nuru alinionyesha gorofa zuri na refu lililo jengwa baharini. Ni jengo zuri ambalo linapendezesha macho ya kila binadamu ambaye atalitazama.

“Ni jengo zuri ehee?”

Nuru aliniuliza huku akiwa amejawa na tabasamu.

“Yaaa ni jengo zuri sana”

Niliitikia kwa unyonge ulio mfanya Nuru kunivuta kidogo na kukilaza kichwa changu juu ya bega leke.

“Jojo ninakupenda sana, ninakupenda sana kuliko kitu chochote”

“Asante, ila hivi kwa nini unanipenda?”

Nilimuuliza Nuru kwa sauti ya upole huku nikimtazama usoni mwake.

“Unajua moyo wangu kwa hapo awali nilihisi kwamba wanaume ndio kila kitu au ndio wanapaswa kupendwa kwenye maisha ya mwanaamke. Maumuvi na visasi ambavyo nilikutana navyo kwenye maisha yagu kipindi nilipo kuwa Tanzania hadi nilipo kuja kuolewa na mwanaume alliye nipita kiumri ila sikuwa ninampenda zaidi ya kupenda mali na pesa zake.”

“Niliishi maisha ya kuutesa moyo wangu kwani mwanaume hakuweza kunitimizia haja zangu za kimwili, hapa ndipo nilipo jikuta nikiingia kwenye mahusiano ya jinsi moja, Nikuwa na amani, ni furaha ikanitawala sana kuwa katika mahusiano hayo. Siku nilipo kuona wewe, japo ulikuwa ni mfungwa tu, ila nilikupenda sana Jojo”

Nuru alizungumza kwa sauti ya upole huku akinitazama usoni mwangu. Nikaona kisiwa kimoja kidogo ila chenye majumba makubwa mawili.

“Pale ndipo ninapo ishi kwa hapa Dubai”

Nuru alinionyesha kisiwa hicho, taratibu helicopter zote zikatua katika kiwanja kikubwa, tukashuka ndani ya helicopter hiyo, tukaingia kwenye gari aina ya Range Rover na kuondoka eneo hili la uwanja wa ndege ndogo.

“Jojo nipo tayari kukupa hata hichi kisiwa, ili kuonyesha kwamba ni jinsi gani ninavyo kupenda, nakuomba usikimbie tena, nakuomba usiwe mbali nami tena. Ninakupenda sana Jojo wangu”

Maneno ya Nuru yakausisimua sana mwili wangu, nikajikuta nikimshika kiuno chake na kuanza kukiminya minya. Tukafika katika moja ya jumba, mlango wa gari hili ukafunguliwa na tukashuka, tukaingia ndani huku Nuru akiwa amenishika kiuno changu, moja kwa moja tukapitiliza hadi chumbani wake. Nuru akanisukumia kitandani na kuanza kuvua nguo moja baada ya nyingine.

“Nuru utaka kufanya nini?”

“Jojo nina hamu na wewe, ni mwaka wa wapili sasa, sijashikwa hata ziwa na wewe, nakuomba Jojo, nakuomba unisaidie mwenzio nina hamu na wewe mpenzi wangu”

Nuru alizungumza akiwa kama amechanganyikiwa, akapanda kiyandani huku akiwa na bikini tu.

“Nakuomba tafadhali”

Nuru alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake. Nuru akaanza kufungua vifungo vya shati langu kubwa nililo livaa. Nilipo litazama tumbo langu hamu yote ya hata kufanya anacho niomba Nuru ikaniishia kabisa, na nikajikuta nikimsukumizia Nuru pembeni hadi akajikuta akianguka chini ya kitanda jambo lililo mkasirisha sana Nuru na akasimama huku akikunya sura yake na ngumi ake akionekana anahitaji kuniadhibu kwa kunipika.



Nuru akaachia msunyo mkali na kuanza kutembea kwa kasi kuelekea bafuni. Taratatibu nikashuka kitandani na kuanza kuzunguka ndani ya chumba hichi kikubwa ambacho kimejaa vito vingi vya thamani kubwa.

“Inabidi ukaoge”

Sauti ya Nuru ikanistua na kunifanya nigeuke na kumtazama, nikamuona akiwa ameshika taulo jeupe, analo litumia katika kujifuta maji katika maziwa yake. Kutokana ninafahamu kwamba nimemuudhi na nimekataa matakwa yake, taratibu nikaanza kuelekea bafuni. Kusema kweli ni bora niwe mpole ili maradi nifanikiwe kumuona mwanangu. Kiumbe ambaye ninamtamani kumuona na ninamsubiria kwa hamu kubwa sana. Ukiachilia mbali baba yake ndio furaha yangu kwake, ila hata huyu mtoto ataongeza furaha mara dufu.

Nikaingia bafuni na kufungua bomba la maji ya mvua, nikamalizia kuvua nguo zangu kisha nikasimama chini ya bomba hili ambalo linwamaga maji mithili ya mvua. Kila ninapo jipapasa na kujishika katika mwili wangu, picha ya Eddazaria inanijia usoni mwangu. Kumbukumbu zangu zinanirudisha katika kipindi ninapo kuwa ninaoga naye.

‘Eddy upo wapi mume wangu, njoo unichukue huku jamani mpenzi’

Nilizungumza kikmoyo moyo huku nikiendelea kuvuta hisia za starehe nilizo kuwa ninazipata kipindi nilipo kuwa na mume wangu. Taratibu nikajishika kitumbua changu na kuanza kukichezea taratibu. Hisia zikazidi kupamba moto na kujikuta nikikiingiza kidole changu ndani ya kitumbua changu na nikashindwa kujizuia kuitoa miguno yangu ya kimahaba.

Kitendo cha kuguswa kushikiliwa kiunoni mwangu, kikanistua sana na kujikuta nikifumbua macho yangu. Nikakutana na Nuru akiwa amejawa na tabasamu. Nuru akaendelea kunipapasa hadi kwenye maziwa yangu na kuanza kuninyonya taratibu taratibu, jambo lililo nifanya hisia zangu kuendelea.

“Aiissiii……”

Nilitoa miguno hiyo mara baada ya Nuru kusimama mbele yangu na kuanza kuninyonya maziwa wangu ambayo kidogo sasa yamejaa kutokana na kujauzito nilio ubeba. Taratibu Nuru akanikalisah katika choo cha kukaa ambacho kimefunikwa na mfuniko wake maalumu. Akanipanua miguu yangu na kuanza kuninyonya taratibu kitumbua changu.

“Ohoo….ais…aaiiiss….Ohoooo”

Miguno ya kimahaba ikazidi kuongezeka katika chumba hichi, Nuru akazidi kuionyesha maujuzi yake ya kuniyonya kitumbua changu. Msisimko ukaongezeka hadi nikajikuta nikifika kileleni. Nikasimama huku miguu ikiyumba yumba kwani nguvu nyingi zimeniishia katika harakati za kupanda kileleni. Nikamkumbatia Nuru kwa sekunde kadha huku nikihema sana.

“Zamu yangu sasa”

Nuru alizungumza huku akiniachia, akainama na kushika choo hichi cha kukaa, nikamtazama kwa muda huku nikijishauri sana kufanya hili jambo. Tartaibu nikaanza kuyatomasa makalio yake malaini.

Nikaanza kumshuhulikia huku nikijitahidi kuhakikisha kwamba ninampatia burudani ambayo itakata kiu yake ya kunitamani kwa kipindi chote hicho. Kutookana ninamjulia na nimemzoea nikahakikisha kwamba nina cheza na kila sehemu ambayo kwake ina hisia kali, hakuchukua muda mrefu Nuru akafika kileleni huku akiwa anapiga mayowe ya furaha na akitoa vicheko vingi sana.

“Nakupenda sana Jojo, wee mtoto unajua kunipagawisha. Unajua ni wapi zilipo ngeg** zangu”

“Kweli?”

“Haki ya Mungu, kwa nini nikudanganye ikiwa huo ndio ukweli halisi, ndio maana nimechanganyikiwa na kupagawa kwa penzi lako. Sinto ruhusu mtu yoyote akuchukua na ukae mbali nami, kwa garama yoyote lazima uzidi kuwa wangu. Kifo sasa ndio kitutengenishe”

‘Ohoo matatizo mengine sasa haya’

Nilijisema kimoyo moyo huku nikimtazama Nuru usoni mwake nikiwa na tabasamu pana sana, ambalo si rahisi kwa Nuru kuweza kufahamu kwamba hayo yote anayo yazungumza ni kwa ajili yake na si kwa ajili yangu na nilazima nitafute namna na jinsi ya kutoroka katika hichi kisiwa.

“Nashukuru kwa kusikia hivyo mpenzi wangu, nitakupenda na kukujalia maisha yangu yote”

“Kweli Jojo?”

“Kweli sihitaji kuwa mbali na wewe sasa”

Nuru kusika maneno yangu ya kumfariji akanikumbatia kwa nguvu.

‘Kuendelea kuishi nawe, ndivyo jinsi nitakavyo hakikisha kwmaba nina kuua, mwana haramu wewe. Sijakisahau kitu ulicho kifanya kwa mume wangu Eddy’

Niliendelea kumuwazia Nuru mambo mabaya huku nikianza kujenga hisia na mipango ya kumuangamiza pale tu nitakapo hakikisha kwamba nimekifahamu kisiwa hichi kuanzia ‘A’ hadi ‘Z’.

“Utamuumiza mtoto”

Nilizungumza huku nikiwa nimejawa na tabasamu.

“Ohoo pole pole jamani mama kijacho”

Nuru alizungumza huku akiniachia. Taratibu akachuchumaa na kuanza kulibusu tumbo langu, mara aliwekee sikio ili maradi ni fujo.

“Natamani mtoto azaliwe wa kike”

“Kwa nini wa kike?”

“Nataka awe jasiri kama wewe”

“Mimi ni jasiri?”

“Sana, tena sana”

“Mmmmm”

“Kweli, ujasiri wako laiti wangekuwa wanao wnaawake wengi hakika wengi wasinge kuwa wanateseka katika ndoa zao na mijiwanaume yao”

“Mmmmm haya”

“Nikuulize kitu?”

“Niulize”

“Hivi yule mwanaume wako ulimpendea nini?”

Nikaka kimya huku nikifikiria ni kitu gani nikijibu.

“Nipo na wewe, sihitaji kuzumzungumzia mwanaume ambaye sihitaji kuwa naye kwenye mapenzi tena”

Nilijikaza sana kuzungumza sentensi hiyo, ila moyoni mwangu kusema kweli ninajihisi msukumo mkubwa wa kusutwa na maneno yangu haya niliyo yatamka, kwani ninampenda sana mume wangu hadi ninahisi kuchanganyikwa.

“Kweli Jojo hauto kuwa naye kwenye mahusiano naye?”

“Asilimia mia moja hata ikitokea leo ninakutana naye hivi sinto weza kuwa naye.”

“Mmmmm kwa nini umebadilisha mawazo yako haraka hivi ikiwa umebeba ujauzito wake?”

“Utamu huu nilio upata leo, kwenye ndoa na wanaume hatuupati. Mwanaume amezoea kukufunua nguo na kukutomb** basi, akimaliza haja zake hakufuti hata shahaw** wake”

Nilizidi kuzungumza maneno ambayo kwa upande mmoja ninaamini ninaanza kumuaminisha Nuru kwamba nipo pamoja naye, ila kwa upande mwengine ninamuomba sana Mungu anisamehe kwani hichi ninacho kizungumza kinaniumiza sana moyo wnagu, na kama mwanangu amepewa uwezo wa kusikia kitu anacho kizungumza mama yake akiwa tumboni basi nina muomba mwenyezi Mungu anisaidie kutomuwezesha kusikia haya matamshi ya kumkebehi baba yake.

“Hapo kweli umenena Jojo, mijiwanaume ipo kwa ajili ya kutimiza haja ya miili yao ila kumjali mwanamke baada ya kugongana ni wagumu sana katika hata kumkumbatia mwenza wake”

“Kweli”

Tukamaliza kuoga na kutoka humu bafuni. Nuru akanitolea gauni jepesi kwenye begi langu na kinikabidhi, nikalivaa. Tukavaa na kutoka ndani humu, Nuru akaanza kunitembeza katika jumba hili lenye mandhari nzuri sana.

“Hiki kisiwa kimezungukwa na papa wengi wakali sana, ambao wanaweza kumarua binadamu kwa dakika moja na hadithi ya maisha yake ikawa imeishia hapo”

“Duuu”

“Yaa”

“Unataka kuniambia hili eneo lote ni la kwako?”

“Yaaa ni langu, nilinunua dola bilioni moja na nusu”

“Duu ni pesa nyingi sana hizo”

“Yaa ni nyingi sana, unajua nipo peke yangu, na pesa zangu huwa sina sehemu ya kuzipeleka”

“Kweli hivi Nuru una utajiri kiasi gani?”

Nilimuuliza Nuru huku tukitembea tembea kwenye fukwe za hichi kisiwa huku walinzi wapatao sita wakitufwata kwa nyuma wakiwa na bundiki zao wakihakikisha kwamba usalama wetu upo vizuri.

“Kwa pesa kama pesa, ukiachilia, majumba makampuni, magari, ndege, meli na boti. Nina utajiri wa dola kama bilioni ishirini hivi.”

“Mmmmmm”

“Yaaa, sasa ukijumlisha vyote hivyo, nipo mbali sana”

“Sasa mbona hata kwenye orodha ya matajiri duniani haupo kwa maana kwa pesa hizo utanakiwa kuwa kwenye chati na kina Bil gate?”

“Hahahaaa Jojo, unajua kuna watu wengine hususani mimi, sipendagi kwanza kujulikama kama ni mtu mwenye pesa nyingi, pili uhalisia wangu unachangia”

“Sijalikuelewa, uhalisia wako kivipi?”

“Yaani Mtanzania, ikija nimetokea kuwa katika head line za matajiri wakubwa duniani, ahaa basi nitaundiwa tume za kuchunguzwa hadi nikome. Na tume hizo hazito kuwa kutoka Tanzania, bali zitakuwa zitatoka mataifa makubwa kama Marekani, unajua watu kama wale huwa wanapenda sana kuona raisi wao ndio wanashikilia kila kitu duniani kama utajiri basi utokee kwao, ikitokea sijui ni Mbongo tena mwanamke ahaaa….watanisaka hadi nijute”

“Duuu kumbe”

“Yaaa ukiwa na mimi nitakufundisha mambo mengi sana, utaweza kufahamu biashara kubwa sana”

Mlinzi mmoja akatembea kwa haraka hadi tulipo akamnong’oneza Nuru sikioni mwake. Nuru akatingisha kichwa chake huku akionyesha swala hilo analitilia mkazo wa hali ya juu.

“Ninakuja”

Nuru alimuambia mlinzi huyo ambaye baada ya kijibiwa hivyo akaondoka katika eneo hili la ufukweni.

“Kuna nini?”

“Ahaaa kuna wageni ambao wamekuja ndio alikuwa ameniambia nikawasikilize”

“Nenda tu kawasikilize”

“No nipo na mpenzi wangu sasa hivi, sihitaji buguza bwana”

“Hapana baby kama ni swala la kibiashara wewe nenda kawasikilize, mimi si nipo jamani”

“Labda twende wote, yaani Jojo, sihitaji kukuacha kabisa, wewe ni mume wangu sasa, popote ambapo utakuwepo na mimi naaka niwepo”

“Mmmm”

“Kweli niamini mpenzi wangu”

Nuru taratibu akaninyonya midomo yangu mbele ya walinzi wake ambao hawajaonekana kishangazwa na kitu cha aina yoyote.

“Haya twende mke wangu”

Nilizungmza huku nikitabasamu. Nuru akanishika mkono na tukaondoka katika eneo hili. Tukaingia katika jumba jengine, tukapitiliza hadi kwenye moja ya ukumbi mmoja mkubwa sana ambao hauna vitu vingi zaidi ya picha picha za baadhi ya viongozi maarufu duniani walio wahi kutokea kama kina Nyerere, Che Guevara na wengine wengi, zikiwa zime bandikwa kwenye kuta za ukumbi huu. Pia ukumbi huu una vinyanga kadhaa vya wajama kadhaa.

“Huu ni ukumbi ambao ni wa kukiri ukweli”

“Ukweli, ukweli kivipi?”

Nuru akatabasamu huku akinitazama. Akapiga mluzi kidogo, mlano mwengine wa ukumbi huu ukafunguliwa, akaingizwa mtu mmoja akiwa amefunikwa uso wake kwa kigunia cheusi, huku akiwa amefungwa pingu mikononi mwake, pamoja na minyororo minene miguuni mwake. Watu wanao muingiza humu mtu huyo ni wanaume wanne wanye miili mikubwa na wamejazia mikono na vifua vyao. Wanaume mmoja akatoa picha ya Nyerere ukutani hapo ndipo nikaona kuna batani kadhaa zilizo kuwa zimefunikwa na picha hiyo. Akaminya moja ya batani, minyoro miwili ikaanza kushuka kutoka juu ya ukumbi huu. Ilipo fika usawa fulani, wakamchukau mtu huyu na kumfunga mwilini mwake.

“Ni nani?”

Nilimuuliza Nuru kwa sauti ya chini.

“Ni mtu ambaye aliniibia mali zangu, sasa leo nimemdaka”

“Ahaaa”

Mwanaume huyo akaminya batani nyingine na kusababisha eneo moja dogo la sakafu ya ukumbi huu kufunguka taratibu. Nikachungulia katika eneo hilo na kuona mambo wakubwa wakiwa wanakatiza chini, jambo lililo yafanya mapigo yangu ya moyo kunienda kasi. Kumbe hili eneo lina mamba wengi hivi. Mwanaume huyu akaminya batani nyingine iliyo isogeza minyororo hiyo iliyo mfunga mtu huyo hadi kwenye eneo hilo la kijikisima kidogo chenye mamba wakali. Kwa ishara Nuru akamuonyesha mwanaume mmoja amvue mtu huyo kigunia hicho. Mwanaume huyo akamsoegelea mtu huyo kwa umakini sana kwani naye akifanya mchezo na mzaha anadumbukia ndani ya kisima hicho. Akamvua mtu huyo kinyago chake, nikajikuta nikishikwa na bumbuwazi kubwa na lenye mshangao mkubwa sana kwani mtu huyu ni Eddazaria, na sikuweza kumfahamu hapo awali kutokana na magunguo aliyo kuwa amevalishwa na yaliweza kuificha kabisa ngozi yake, ambayo naamini kama ningeweza kuiona hapo awali basi ningeweza kumtambua hata kabla hawajamuweka usawa wa kisima hicho cha mamba.



Tukatazamana na Eddazaria kwa sekunde kadhaa. Machozi yakaanza kunilenge lenga. Nuru akanitazama huku akitabasamu.

“Tumekutana tena leo Eddy”

Nuru alizungumza kwa sauti iliyo jaa dharua ndani yake huku akinisogelea. Akanishika kiono changu jambo lililo nifanya nifumbe macho yangu kwa uchungu sana, kwani nikifanya kosa lolote tu ninakwenda kumpoteza Eddazaria wangu.

“Uliniibia mpenzi wangu, msichana ninaye mpenda sana, Jojo ndio kila kitu changu, ulihisi kwamba siku sinto kuja kukutia mikononi tena?”

Nuru alizungumza huku akiendelea kunipapasa papasa kwa mkono wake wa kushoto kwenye maziwa yangu jambo lililo nifanya nizidi kuchanganyikiwa kwani kiu ninacho fanyiwa mbele ya mume wangu kwa kweli kinaumiza. Nuru hakuishia hapo, akanishika mashavu yangu na kuanza kuninyonya lispi zangu taratibu. Nikamshuhudia Eddazaria akimwagikwa na machozi usoni mwake, nikatamani kumsukuma Nuru ila mikono ikakosa nguvu kabisa kwani sehemu ambayo Eddazaria yupo ni sehemu ya hatari sana.

“Unaona, unaona Jojo ananipenda mimi kuliko wewe mshenzi”

Nuru alizidi kuzungumza kwa kejeli kubwa iliyo nifanya nizidi kuumia moyoni mwangu.

“Leo ni muda wa kufa kwako. Jojo nikuulize kitu?”

Nikaka kimya kwa sekunde kama tano kisha nikatingisha kichwa changu nikimuomba niulize hicho alicho kifapanga kuniuliza mimi.

“Unanipenda?”

Nikamtazama sana Eddazaria, swali la Nuru najua ni mtego mkubwa sana kwake.

“Ndio ninakupenda”

“Kama nani?”

“Mke wangu”

“Waoooooo”

Nuru akanikumbatia kwa nguvu, kwani kila swali alilo niuliza ni swali la mtego.

“Mshusheni aliwe na mamba”

Mwanaume huyo akaminya batani na kuifanya minyororo hiyo iliyo mshikilia Eddazaria kuanza kuelekea chini alipo Eddazaria

“Acheni”

Nilizungumza kwa sauti ya upole huku nikikimbilia katika kisima hicho cha mamba. Nikasimama karibu kabisa na kisima hicho huku nikurudi nyuma nyuma.

“Nuru kwa nini unavunja makubaliano yetu, kwa nini hutaki kuelewa, nimekuambia ninaye kupenda ni wewe kwa nini unataka kumtesa Eddazaria wa watu pasipo sababu yoyote eheee?”

Nilizungumza huku nikilia kwa uchungu mwingi sana. Nuru macho yakamtoka, kwa ishara akamuamuru mwanaume huyo kusitisha zoezi la kutaka kumdummbukiza Eddazaria katika kisima hicho cha mamba.

“Kwa nini lakini huwi muelewa. Muachie kaka wa watu aondoke, nimesha sema kwamba sinto rudiana naye kwa nini huamini, kwa nini hutaki kuelewa jamani”

‘Jo..o…”

Eddazaria alizungumza kwa shida sana, na anaonyesha dhairi kwamba amepigika sana toka huko alipo tolewa.

“Nakupenda wewe tu Nuru”

Nilizidi kuzungumza maneno ambayo nina imani kwamba yana ufanya moyo wa Eddazaria kuumia kwa maumivu makali sana. Nuru akanitazama kwa macho makali ambayo nina imani hichi ni kipipo dhairi cha kupima upendo wangu kwake.

“Kama huamini kwamba ninakupenda Nuru, ni bora nijue mimi wote munikose”

“Hapana, hapana Jojo”

Nuru alizungumza huku akiwa amejawa na wasiwasi mwingi sana, kwa haraka kisima hichi kikafungwa. Nuru akanifwata sehemu nilipo simama na kunikumbatia kwa nguvu huku machozi yakimwagika.

“Jojo upo tayari kunioa?”

“Nipo tayari ila ninakuomba umuachilie Eddazaria aondoke zake”

“Kweli”

“Haki ya Mungu, ninakuomba umuache aondoke, sihitaji mtu yoyote sasa hivi aumie kwa ajili yangu, sihitaji Eddy afe kwa ajili yangu muachie na huu ndio uwe mwisho wa malumbano kati yenu”

Nilizidi kuzungumza kwa uchungu, sehemu ambayo Nuru aliishika kwa kweli ni mbaya sana, sina ujanja na wala sina uwezo wa kumsaidia Eddazaria wangu zaidi ya mimi mwenyewe kujitoa sadaka kwa upande wa Nuru kwa maana yeye ndio mwenye nguvu kumliko hata mume wangu.

“Kwa hili nitakuachia huru wewe nguruwe, ila ole wako ujaribu kufanya ujinga wa kumtafuta Jojo, nakuhakikishia kwamba ni lazima nitakuua, tena nitakuua kwa mkono wangu mimi mwenyewe, nitakuchinja kama kuku sawa”

Nuru alizungumza kwa ukali huku akimtazama Eddazaria anye lia kwa hasira sana, kwa maana nina muelewa vizuri tena vizuri sana. Wakamshusha Eddazaria sehemu waliyo kuwa wamenining’iniza, wakamfungua minyororo, kitu nilicho kigundua wamempiga hana hata uwezo wa kusimama.

“Naomba nizungumze naye”

Nilizungumza kwa ujasiri na msisitizo huku nikimtazama Nuru usoni mwake. Nuru kwa aisha akawaomba vijana wake watoke nje kisha yeye akasimama mbali na sehemu tulipo. Kilio cha maumivu makali kikaanza kutawala katikati yetu, katika maisha yetu ya furaha na amani hatukutarajia kama ipo siku mwisho wetu utakuja kuishia kama hivi. Moyo wangu unampenda na yeye natambua kwamba ananipenda ndio maana kila anacho kifanya ni kwa ajili ya upendo wake kwangu, ila sitaki tena ateseke na kuumia kama hivi.

“Eddy”

“Mmmmm”

“Nashukuru kwa kila kitu, nashukuru kwa kila ulilo nifanyia. Wewe ni mwanaume wa ajabu sana. Mwanaume uliye yahatarisha maisha yako kwa ajili yangu, mwanaume ambaye unapambana kwa ajili ya upendo wako kwangu…..”

Nikameza mate kidogo huku nikiendelea kumwagikwa na machozi.

“Najua unanipenda, najua unazidi kunipenda najua hilo Eddy, ila sasa nakuomba Eddy nakuomba Eddy……..”

“Nakuombe MPENZI YETU YAISHI HAPA”

Maneno manneya mwisho niliyo yazungumza yakamfanya Eddazaria kunitazama kwa mshangao huku macho yakiwa yamemtoka, akajaribu kunishika uso wangu, ila nikauwahi mkono wake na kuushusha chini.

“Sihitaji kuwa na wewe tena Eddy, ni wakati wa wewe kuwa na familia yako, ni wakati wa wewe kuwa na mwanamke uliye zaa naye mtoto wako wa kwanza, nenda tu kwa mama Gody ila mimi nakuomba uniache”

“Hapana…..hapana Jojo unanidanganya, sema kama unanidanganyaaaa”

Eddazaria alizungumza huku machozi yakizidi kumwagika usoni mwake.

“Sikudanganyi Eddy na sahau kama ulisha wahi kuwa na mahusiano na mtu kama mimi, sahau kabisa, pia huu ujauzito sio wa kwako. Siku zote nilikuwa ninakudanganya, siku zote nilikuwa nina kuongopea moyo wako. Nisamehe”

Nilizidi kuzungumza maneno ya kumkatisha tamaa Eddazaria, maneno ambayo sidhani ambayo sidhani kama kuna mwanaume angefurahi kuyasikia kutoka kwa mwanamke ambaye alisha muwekea malengo kwenye maisha yake.

“Jojo unananidanganya, Jojo unaniongopeaa”

“Huo ndio ukweli, sahau kama nilikuwa na mimba yako, hii mimba ni ya daktari mmoja, daktari aliniingilia kimwili na nikashika ujauzito wake, ila si wa kwako”

Eddazaria akanishika mashavu yangu kwa nguvu huku mikono yake ikimtetemeka kwa jazba kubwa sana. Nikamuoan Nuru akija kwa haraka kwani kwa kushikwa huku kuna wea kupelekea hata kuuwawa na mwanaume huyu. Nikamzuia Nuru kwa ishara ya mkono hatua chache kabla hajatufikia na kweli Nuru akatii nilicho muambia na akasimama.

“Jojo niambie kwamba ninaota. NIAMBIEEEEEEEEE……..!!!”

Eddazaria alizungumza huku akinitingisha kichwa changu kwa nguvu sana. Nywele zangu kichwani zikachanguka changuka.

“Huoti Eddy huo ndio ukweli, rudi Tanzania ukaendelee na maisha yako. Mimi ni mwanamke mbaya mimi ni msagaji, mimi sijazoea kutomb****. Nimezoea kunyonya kum** za wanawake wezangu, niache, niache Eddy”

Eddazaria akaniachia mashavu yangu huku akiwa na bumbuwazi kubwa, akaaanza kuachia kicheko kikali huku akitutazama mimi na Nuru. Kicheko cha Eddazaria kikazidi kuniumiza moyoni mwangu kwani ninatambua kwa maneno yangu na taarifa hii imemfaya kuanza kuchanganyikiwa.

“Ombi moja la mwisho kwako, Eddy kaa mbali na mimi”

Baada ya kumaliza kuzungumza maneno hayo nikasimama na kumtazama Nuru, nikamuona akiwa amejawa na tabasamu. Nikapiga hatua chache hadi sehemu alipo simama.

“Nimefanya haya yote kwa ajili yako, ninakuomba sasa umrudishe Eddazaria Tanzania, mrudishe akiwa salama na aendelee kufanya kazi zake zitakazo muingizia kipato sawa”

“Nakuahidi mume wangu, nitafanya utakavyo”

Nuru alizungumza huku uso wake ukiwa umetawaliwa na furaha. Ila furaha hii naamini ipo siku moja itakuja kuwa kilio cha kusaga meno kama jinsi leo nilivyo mliza Eddazaria wa watu ambaye naamini kwamba anajutua ni kwa nini amenifahamu mimi.

“Na kingine, nahitaji umapatie kiasi cha pesa kitakacho mtosheleza katika maisha yake”

“Usijali mume wangu”

Nuru akapiga mluzi tena na watu wake wakaingia, Nuru akawanong’oneza.

“Nataka nisikie unawaambia nini?”

Nilizungumza kwa sauti huku nikiwatazama wanavyo nong’oezana.

“Jamani baby umesha anza kuwa na wivu leo tu, ninamuambia kwamba aandae private jate itakayo mpelekea Eddazaria hospitalini hapa hapa Dubai, kisha apelekwe nyumbani Tanzania, au nimefanya vibaya mpenzi wangu?”

Nuru alizungumza kwa sauti iliyo mlegea kidogo, ni mwana mama ila anapenda sana mambo ya usichana na ya ajabu kupindukia.

“Jojo kwa hili sinto kusamehe hadi kufa kwangu, sinto kusamehee Jojo”

Eddazaria alizungumza huku akiburutwa na walinzi hawa. Wakatoka ndai ya ukumbi huu, machozi yaliyo kuwa yamekatika kwa muda yakaanza kuchuruzika tena usoni mwangu. Kwani kwa mara ya kwanza sasa nimeingia kwenye uaduia na mwanaume ambaye ninampenda sana, ila sina jinsi ninafanya yote haya ni kwa ajili ya mwanangu aliyopo tumboni, laiti ningekuwa sina huu ujauzito basi ningeweza hata kupambana na kurusha mateke mawili matatu.

Nikatoka humu ndani na kukimbilia katika jumba jengine ambalo lina chumba chetu cha kulala, moja kwa moja nikaeleke hadi chumbani huku Nuru akiwa ananifwaya kwa nyuma.

“Jojo ila maamuzi uliyo yafanya ni mazuri sana”

“Nuru nahitaji kuwa peke yangu kwa sasa sawa”

Nilizungumza kwa ukali huku nikiwa nimesimama hatua chache kabla ya kuuifikai mlango wa kuingia ndani ya chumba hichi cha kulala. Nuru akanitazama kwa muda kidogo kista akatinngisha kichwa chake ikiwa ishara ya kunikubalia kwamba niwe peke yangu. Nikafungua mlango wa chumba hichi na kuubamiza kwa nguvu. Moja kwa moja nikapitiliza hadi bafuni, nikaingia ndani ya sinki la kuogea na kuangua kilio kizito na kikali sana.

“Kwa nini mimi, kwa nini mimi lakini, nina mikosi gani kwneye maisha yangu jamani akhaaa?”

Nilizungumza huku nikiwa ninalia kwa uchungu sana, maamuzi kama haya sikuyatarajia wala kutawazia kwenye maisha yangu kwamba ipo siku nitakuja kuyafikia na kiyafanya kwa yule nimpendaye, aliye jitolea maisha yake kwa ajili yake.

“Eddy nisameheeee, Eddy sitaji ten aufe kwa ajili yangu”

Nilizungumza kwa uchungu sana huku nikiwa nimejikunyata ndani ya sinki hili.

‘Jojo kwa hili sinto kusamehe hadi kufa kwangu, sinto kusamehee Jojo…………………..’

Maneno ya Eddazaria yakakatiza katika kichwa changu na kujikuta nikizidi kulia kwa uchungu sana.

‘Lazima mwanangu uwe hai, ukiwa hai ni lazima huyu shetani nimuue, sasa hivi vumilia, vumilia baba yako nimemuacha si kwa kupenda, ila nimemuacha kwa ajili ya usalama wake, nisamehe mwanangu’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikilishika tumbo langu hili. Nikaka humu bafuni kwa muda mrefu hadi usingizi ukanipitia na nikalala fofofo.

“Jojo, Jojo, Jojo”

“Ehee…..”

“Amka mpenzi wangu”

Nikafumbua macho yangu na kukutana na sura ya Nuru, nikatamani umtukana ila nikajizuia kwa maana sasa hivi ninatakiwa kuwa mvumilivu ili Eddy na familia yake waendelee kuwa salama. Taratibu Nuru akaninyanyua na kutoka katika hili sinki la kuogea, tukatoka humu bafuni huku akiwa amenishika mkono.

“Sasa hivi ni saa ngapi?”

“Saa nne usiku, twende tukapate chakula cha usiku”

Nuru alizungumza huku akiwa amejawa na tabasamu kubwa sana. Kwa ishara ya mkono nikamuomba tuelekee katika meza hiyo ya chuakula.

“Ulifanya kama nilivyo kuambia wapi mumpeleke Eddazaria?”

“Ndio, amesha patiwa matibabu na sasa ndege ipo njiani inampeleka nchini Tanzania. Yaani Jojo katika siku zote za maisha yetu ulizo wai kunifurahisha ni leo mpenzi wangu”

Maneno ya Nuru yakazidi kuniumiza kwa kweli, kwa maana furaha ambayo ipo kwake leo, kwa upande mwengine ni huzuri kwa baba wa mwanangu ajaye.

“Yaani nimesha zungumza na mchunguji pamoja na marafiki zangu wengine na nimewaambia kwamba kesho ni siku ya hasusi yetu mimi na wewe”

Nikastuka sana kusikia neno mchungaji.

“Unataka kusema mchungaji atatufungisha ndoa ya jinsi moja?”

“Ndio mbona umestuka, au hujui kama siku hizi ndoa ya jinsi moja hufungishwa hata makanisani ila mimi sijapenda niifungie kanisani zaidi ya hapa nyumbani kwangu, naamini kesho upo tayari kwa ajili ya kunio?”

‘Sijui kama kesho utaifikisha kwa maana usiku wa leo lazima nikuue sihitaji kuingia kwenye aibu ya dunia kwa kufungishwa ndoa ya jinsia moja’

Niluzumza kimoyo moyo huku nikiwa nimejawa na tabasamu na jicho langu moja la kuiba ninatazama kisu kikali kilichopo kwenye meza ya chakula kinacho tumika kumenyea matunda, na nina imani kwa kupitia kisu hicho hichi, basi leo ndio kitayafikisha maisha ya Nuru mwishoni mwake kwa kulichinjilia mbali koromeo lake.



Nuru taratibu akakivuta kiti kimoja nyuma, kwa ishara akaniomba niweze kukaa kwenye kiti hicho, macho yangu yote bado nimeyapeleka kwenye kisu, huku kichwani nikiendelea kujenga picha ya tukio la kumuangamiza Nuru jinsi itakavyo kuja kuwa.

“Baby, Baby”

“Mmmmm”

Nilistuka kidogo mara baada ya Nuru kuniiita huku akinitingisha.

“Kaa jamani mpenzi wangu, una mawazo gani?”

“Aha..hamna”

Nilizungumza huku nikikaa kwenye kiti hichi, Nuru akazunguka upande wa mbele wa meza hii, akavuta kiti chake na kukaa kitako. Akaanza kufunua sahani zilizo funika vyakula vilivyo andaliwa.

“Usiku huu wa leo kwangu ni usiku wenye furaha sana”

Nuru alizungumza huku akiwa amejawa na tabasamu pana usoni mwake. Nikatabasamu tu huku akilini mwangu nikijitahidi kupanga na kupangua ni kitu gani ambacho ninaweza kukifanya juu ya kumuangamiza Nuru.

“Jojo, Mungu bariki mwanao akizaliwa, nitamrisisha asilimia sabini na tano ya utajiri wangu wote, yeye ndio atakuwa ndugu wa pekee na mrithi wa utajiri wangu”

Maneno ya Nuru kidogo yakafuta mipango ya kumuua, nikajihisi kama furaha ikitawala katika moyo wangu.

“Kweli?”

“Ndio, nitampa utajiri wangu mara tu atakapo zaliwa. Unajua umri umesha kwenda sasa, siku yoyote ninaweza kufa. Kifo changu nahitaji kiwe na faida kubwa kwako. Sihitaji nife uje kusumbuliwa, na watu wengine ambao wana uchu wa mali zangu”

Maneno ya Nuru yakazidi kusogeza kando harakati na mipango yangu ya kumuangamiza na tayari amesha anza kujitabiria kifo.

‘Una bahati sana umemuhusisha mwanangu kwenye mipango yako la sivyo, leo haitakwisha kwenye maisha yako’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikiendelea kumtazama Nuru usoni mwake.

“Ila kwa nini unahisi utakufa”

“Ahaa…kila binadamu ni lazima afe, ila je atakufaje hapo ndipo kwenye mtihani. Apo awali nilipo kuwa na uadui na wewe nilijua kwamba wewe ndio utakuja kuniua”

Nikastuka kidogo, kwani Nuru anazihidi kuzikaribia hisia zangu mbaya nilizo zijenga kichwani mwangu.

“Ila kwa sasa sidhani kama utaweza kuniua tena, umedhihirisha ni jinsi gania mbavyo unanipenda na ni kweli unanipenda”

“Yaa ninakupenda”

Nilizungumza kitafki tu ili mradi kunogesha mazungumzo haya. Tukamaliza kula chakula kutokana leo ilikuwa ni siku ndefu na siku ambayo kwa namna mmoja ama nyingine iliwa ni ndefu sana kwetu, tukalala usingizi fofofo. Alfajiri na mapema nikawa ndio mtu wa kwanza kuamka kati yangu mimi na Nuru. Nikavaa dera langu na kutoka chumbani humu, nikafika sebleni, nia na lengo langu la kuamka asubuhi kama hivi ni kuhakikisha kwamba nina pata simu, nitakayo weza kuwasiliana na mdogo wangu Judy, kwani sijui hadi sasa hivi ana hali gani kwenye maisha yake.

“Hei”

Nilimuita mlimzi mmoja niliye mkuta mlangoni akiwa amesiamama huku ameshika bunduki yake, akanisalimia kwa heshima huku akiinishamisha kichwa chake kidogo, japo ni mtu mzima na mwenye uwezo hata wa kunizaa mimi, ila heshima aliyo nionyesha ni kubwa sana na ninatambua kwamba ni heshima itokanayo na pesa za Nuru anazo lipwa.

“Ahaa, ninaweza kupata simu?”

“Hapana huwa tatutumia simu, zaidi ya hizi simu za upepo ambazo hutoa mawasiliano hapa hapa ndani ya kisiwa hichi”

“Kwa nini?”

“Ndio utaratibu ulipo madam”

Kauli ya mwanaume huyu kidogo ikanikagtisha tamaa katika utafutaji wangu wa simu, nikarudi katika chumba cha kulala na kumkuta Nuru akijigeuza geza kitandani. Nikajilaza pembeni yake, taratibu nikamshika bega lake na kuanza kumtingisha kidogo.

“Mmmm”

“Kumekucha”

“Kweli baby?”

“Yaa kumekuacha amka”

Nuru taratibu akanisogelea na kuninyonya lispi zangu taratibu.

“Baby nahitaji simu”

“Simu”

“Eheee”

“Ya nini?”

“Nahitaji kuwasiliana na mdogo wangu”

“Aha..nimesahau jana kukuambia. Mdogo wako yupo njiani anakuja huku Dubai, naye niliamua kumchukua ili uwe na amani unapo kuwa karibu naye”

“Mmmmm”

“Mbona unaguna hau ujafurahi?”

“Umemchukua chukuaje?”

“Kwa njia ya amani kabisa na yupo kwenye ndege yangu binafsi, majira kama ya saa nne hivi watatua hapa katika kiwanja cha ndege”

Sikuwa na neno la kuzungumza zaidi ya kukaa kimya kabisa. Tukaendelea kujilaza hapa kitandani huku kwa mara kadhaa Nuru akianza uchukozi wa kunishika shika mwili wangu ili kuzifanya hisia zangu ziweze kuamka.

“Nuru”

“Beee”

“Unaonaje harusi yetu tukaisogeza mbele hadi pale mwanangu atakapo zaliwa?”

“Haiwezekani mpenzi wangu kwani kila kitu nimesha kipanga na ninasubiria tu mdogo wako aweze kufika na shamra shamra zianze kupamba moto, kwa maana harusi itakuwa ni usiku”

Nikakaa kimya kwa muda huku nikimtazama Nuru usoni mwake.

“Nikuombe kiti kingine?”

“Niombe tu mpenzi wangu”

“Unaonaje katika harusi yetu pasiwepo wachukua video wala watu kuingia na simu zao za kamera wala wapiga picha”

“Kwa nini unasema hivyo?”

“Basi tu”

“Mpenzi wangu ni lazima tuweke kumbukumbu ya penzi letu, video na picha hivyo vitakuwepo mpenzi wangu, ila mbona una wasiwasi mwingi ikiwa umenidhibitishia kwmaba nipo tu mimi peke yangu kwako au kuna mwengine?”

“Maana yangu sio hiyo”

“Ila?”

“Ila ninahofu na mashaka juu ya watu huko nje watatuchukuliaje, na kumbuka kwamba filamiu bado haijatoka?”

“Hilo la filamu wala lisikupe shida, ataitoa Eddy, hilo ndio litakuwa jukumu lake sasa, na usiwazie kuhusiana na filamu hiyo kwa maana pesa ambazo utazipata hata hiyo filamu haito ingiza kiasi kama hicho cha pesa”

“Nuru…..”

“Ndio Jojo, pesa, pesa ndio kila kitu kwenye maisha yako. Kumbuka kitu ambacho kilikupeleka chini kwa mara ya kwanza. Ulihatarisha maisha yako kwa ajili ya pesa. Kwa nini leo unaikataa pesa ambayo mimi ninakupatia eheee?”

Nuru alizungumza kwa msisitizo na kwa hasira kidogo jambo lililo nifanya nikae kimya kwa muda. Ni kweli kila binadamu kwenye maisha yake anahitaji pesa, na kila mtu ana njia yake ya kutafuta pesa. Ikiwa mwanangu amesha pata uhakika wa utajiri hapo mbeleni, sina budi ya kukaa kimya na kukubaliana na matakwa ya Nuru.

Masaa yakazidi kuyoyoma, tukapata kifungua kinywa na majira ya saa tano kasoro ndege ndogo ya kifahari ikatua katika kiwanja cha ndege kidogo kilichopo katika hili eneo la kisiwa. Judy akashuka kwenye ndege hiyo huku akiwa ameongozana na wadada wawili walio valia suti nyeusi. Judy kwa haraka alipo niona akanikimbilia na kunikumbatia kwa nguvu, taratibu akajikuta akiangua kilio kikali huku akizidi kunikumbatia, kwani ni mwezi wa pili sasa mimi na yeye hatujaonana.

“Nilijua umekufa dada yangu”

“Sijakufa Judy”

“Ilikuwaje kuwaje ukaokoa kwenye ile ajali?”

Judy aliniuliza huku akiendelea kulia na kuzidi kunikumbatia.

“Usijali tutazungumza, sawa mdogo wangu”

Taratibu Judy akaniachia huku akitingisha kichwa akimaanisha kwamba amekubaliana nami. Nikamtambulisha Judy kwa Nuru, kisha tukaingia kwenye gari ambalo tumekuja nalo hapa katika uwanja huu wa ndege ambao upo mbali kidogo na jumba tunalo ishi.

“Dada huku ni pazuri, nimepanda kwa kweli”

“Kweli?”

“Haki ya Mungu vile, kisiwa hichi kinaitwaje?”

“Jojo”

Nuru aliwahi kujibu na kutufanya tumtazame kwa mshangao kwa maana yeye amekaa siti ya mbele pamoja na dereva.

“JOJO…….!!?”

“Ndio, au hujapenda kiitwe jina la dada yako?”

“Ahaa nimependa kwa maana dada yangu ni maarufu”

“Yeeha basi hichi kisiwa ndio jina lake”

“Safi, ehee niambie naona tumbo linakua dada yangu?”

“Yaaa Mungu asaidie nijifungue salama”

“Kweli, bibi yake ana huzuni kama nini?”

Ikabidi nimwahi kumfinya Judy kwenye paja lake pasipo hata Nuru kuaona kwa maana hadithi ambayo Judy anataka kuileta hapa kusema kweli itaweza kuleta matatizo mengine ambayo sihitaji niweze kuyapata wala kuyasikia wa muda huu.

“Kampuni uliisimamia vizuri?”

Ilibibidi nibadilishe mada ya mazungumzo.

“Yaa inakwenda vizuri, kuna filamu moja niwemwaacha wanaitengeneza siku si nyingi itatoka?”

“Ni nzuri?”

“Nimepita mule mule kwenye filamu kama yako ya mwanzo, ila nimeshirikisha wananii marufu kutoka Marekani”

“Kutoka Marekani, imemchukua nani na nani?”

“Jonson Stathan na Kalvin Hart”

“Duuu”

“Yaa humo ndani utaipenda”

“Umewapataje pataje hao watu?”

“Unajua ile kampuni muliiachia matawi mazuri, matawi ambayo mtu unaweza ukafika juu kwa jinsi mwenyewe unavyo penda, wale watu wa Universal studio ndio walinisaidia kuniletea hao waasanii, hadithi ikatungwa na Mmarekani, yaani wee acha tu, huku nimekuja kukaa siku mbili hizi kisha narudi zangu Tanzania”

Nuru akageuka na kututazama huku akitabasamu, kwa jinsi anavyo onekana swala la Judy kurudi Tanzania nahisi halito wezekana.

“Kumbe na wewe ni kichwa kama dada yako?”

“Hahaa, baba mmoja, mama mmoja ni lazima wazae watoto ambao ni Genius, ila mwanzoni tulionekana mazoba kutokana na pesa. Pesa hatukuwa nayo ndio maana tukaonekana kwamba hatuna maana kwenye jamii ambayo tulikuwa tunaishi”

Judy kusema kweli amekuwa muongeaji sana, sijui ni kutokana na furaha ya kuniona mimi au kuna jambo jengine zaidi ya hilo. Tukafika katika jumba tunalo ishi, tukawakuta wapambaji wakiendelea na heka heka zao za kupamba kila eneo hii jumba ili harusi yangu mimi na Nuru izidi kupamba moto.

“Mume niandalia jamani sherehe nini?”

Judy alizungumza huku akishanga shangaa jinsi watu hawa wanavyo pamba.

“Yaaa, ni sherehe ya kukubaribisha nyumbani”

Nuru alijibu na kunifanya nimtazama kwa jicho kali kidogo.

“Ohoo jamani asante, shangazi asante pia”

Judy alizungumza hukua kimkumbatia Nuru kwa nguvu. Akamuachia hukua kiwa amejawa na tabasamu.

“Usijali Judy”

Tukaingia katika chumba ambacho Judy atamkitumia kuingia ndani. Akaanza kushangaa shangaa chumba hichi kilicho pangiliwa vizuri.

“Waoooo, dada hichi chumba nimekipenda kwa kweli”

“Etii eheee?”

“Yaa nimekipenda sana jamani”

“Jojo ninakwenda kuwasimamamia watu hawa waweze kupanga kuna urembo nahiji wauweke”

Nuru alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.

“Sawa”

Nilijibu kinyonge na Nuru akatoka chumbani humu, nikaufunga mlango kwa ndani kisha nikapiga hatua za haraka na kumkumbati Judy na kuangua kilio upya. Judy akabaki kimya akinisikilizia jinsi ninavyo lia, kwani kama ni kulia tulisha lia kipindi tunaonana katika kiwanja cha ndege, swala naamini analo jiuliza ni kwa nini nina lia sasa hivi.

“Jojo”

“Mmmmmm”

“Kwa nini un alia”

Taratibu nikamuachia Judta na kukaa kitandani na kumfanya na yeye akae huku akinichunguza machoni mwangu kwa umakini mkubwa sana.

“Jojo niambie nipo hapa mdogo wako, kumbuka mimi ndio ndugu yako niambie unalia nini?”

“Nimeachana na Eddy”

“Umeachana na Eddy kivipi, kwani ulionana naye?”

Swali la Judy likanifanya machozi yazidi kumwagika usoni mwangu. Nikamshika vinanja vya mikono yake na kuanza kuviminya minya.

“Mimi na Eddy hatupo kwenye mahusiano tena, nimeachana naye moja kwa moja.”

“Kwa nini?”

Judy aliniuliza huku uso wake ukianza kutawaliwa na ndita nyingi usoni mwake, inaonyesha dhairi kwamba hii habari hajaipenda kuisikia kwa muda huu.

“Jojo niambie kwa nini umeachana na shemeji?”

“Kwa sababu…..kwa sababu…..”

“Kwa sababu gani, niambie”

“Nahitaji, nahiyaji KUOAA”

Judy taratibu akaviachanisha vinganja vyake na viganga vyangu, akasimama huku uso wake ukiwa umejaa mshangao na ndita nyingi sana, huku mashangao ukiwa umemtawala usoni mwake.



“Hahaaa, Jojo nimesikia vibaya au?”

Judy alizungumza huku akicheka, jambo lililo nifanya nishushe pumzi nyingi kwani nilicho muambia nina imani kwamba kitakuwa ni ngumu kwa yeye kuweza kukielewa.

“Judy njoo ukae hapa”

“Siwezi kukaa ikiwa unaniambia vitu ambavyo havieleweki, niambie kitu cha kueleweka Jojo ili nikuelewe”

Judy alizungumza kwa ujasiri sana, kana kwamba mimi na yeye, yeye ndio mkubwa kwangu.

“Ndio nataka kumuoa Nuru”

“What…...?”

“Ndio, nahitaji kumuoa Nuru”

Nilizungumza kwa jazba huku machozi yakinimwagika usoni mwangu. Judy taratibu akarudi nyuma nyuma na kukaa kwenye sofa lililopo humu ndani huku akinitazama usoni mwangu.

“Kumbe yale maneno ya usagaji yaliyo kuwa yakizungumwa na watu kumbe ni kweli si ndio?”

“Ndio mimi ni msagaji”

“JOJO NI USENG** GANI UNAUZUNGUMZA DADA YANGU UNA NINI LAKINI WEWEEE. HUNA HATA HAYA UNAJIBU KABISA KWAMBA WEWE NI MSAGAJI………….”

Judy alizungumza kwa sauti ya juu huku akinyanyuka na kunifwata kwa haraka kwenye kitanda nilicho kaaa. Nikasimama kabla hajafika, tukatazamana huku machozi yakitumwagika kwenye macho yetu.

“Wewe unahisi utajiri wote nimeutoa wapi, Unajia ni jinsi gani nilivyo pitia shida nikitafuta pesa maisha yetu yawe mazuri hivi eheeee?”

“Sina haja ya kujuaa laana zako, kama ni utajiri wako uliutafuta kwa kusagana ni wa kwako, na sikukutuma ukasagane ili upate utajiri sawa?”

“Hahahaaaa……leo hii unavaa vizuri, unaweka nywele zako vizuri ndio unaona kwamba nilicho kifanya ni kibaya si ndioo?”

Nilizungumza huku nikizishika nguo za Judy pamoja na kwenye zake, akaitoa kwa nguvu mikono yangu.

“Don’t ever try to touch my body again…….”(Usidhubutu kuugusa mwili wangu tena)

Judy alizungumza kwa kufoka huku akinikazia macho na kunisogelea karibu kabisa. Nikamtandika kofi zito lililo mfanya atazame pembeni kwa muda huku sauti ya meno yake jinsi yanavyo jing’ata kwa nguvu ikisikika. Taratibu akanitazama huku machozi yakiendelea kumwagika usoni mwake.

“Piga tena na huku”

Judy alizungumza huku akinielekezea shavu la upande wa kushoto, nikampiga kofi jengine lililo zito, akajiweka sawa na kwa ishara akaniombe nimpige kwa mara nyingine kwenye shavu la upande wa kulia. Nikamtandika kofi jengine zito hadi akayumba yumba na kusoegea mita chache kutoka nilipo simama.

“Jua kwamba mimi ni dada yako, mama kipindi alipo kufa alikuacha bado unajinyea na kujikojolea mpuuzi wewe. Nilipambana kuhatarisha maisha yangu kwa ajili yako, kama ningekuwa peke yangu ni bora hata ningekuwa malaya wa kujiuza Sinza kama wanavyo jiuza malaya wengine ila nilifanya yote ili uwe na maisha mazuri mjinga wewe”

“Kwa hiyo kujinyea kwangu na kujikojolea ndio kumekufanya ukawe msagaji si ndio?”

“Ndio”

“Ahaaa…..sasa sikia ni hivi. Kuanzia hivi sasa hivi mimi sio ndugu yangu yako. Sahau kama ulishwa wahi kuwa na mdogo wako anaye itwa Judy. Kila mtu aishi maisha yake, nitarudi Tanznaia na nitakwenda kuitafuta pesa yangu hata kwa kuuza mchicha.”

Judy alizungumza huku akiifwata pochi yake mezani, akaichukua na kaunza kutembea kuelekea mlangoni huku akiwa amefura kwa hasira sana.

“JUDY, JUDY”

Judy akageuka na kunitazama.

“Komba kuniita Judy. Shetani mkubwa weweee, dini zote zinakataza juu ya usagaji ila wewe unaendekeza etii ohooo umefanya kwa ajili yangu, nilikutuma ukawe msagaji. Tena uanakuwa msagaji na jimama ambalo linataka kumtoa mtoto wa watu maisha yake yote kwa ajili yako, ila wewe huliewewi hilo zaidi ya kulete useng** wako.”

Judy alizungumza huku akiwa amekasirika sana.

“Jua haya machozi tunayo lia mimi na Eddazaria ni lazima yatawarudia wajinga nyinyi. Sasa hivi kuna mwanaume anaweza kujitoa kwa hali na mali, hata kuhatarisha maisha yake mwisho wa siku unakujua kumuacha, laana haitoki kwa mama wala baba tu, ila hata mimi ninakuachia laana na kama huyo mtoto ni mali ya Eddy maze na umeidishe kwenye familia ya watu na wewe uendelee na ushetani wako”

Maneno ya Judy kusema kweli yanaumiza sana moyo wangu, kwani huyu ndio ndugu yangu wa pekee kabisa na ndugu ambaye kusema kweli sina mwengine zaidi yake. Judy akafungua mlango na kutoka ndani humu na kuubamiza mlango kwa nguvu.

‘NO’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikiaanza kutembea kuelekea nje, nikamuona Judy akikunja kona na kuelekea kwenye ngazi zilizopo katika gorofa hili. Nikaanza kumkimbilia, huku nikimuita kwa nguvu.

“Nini?”

Judy alisimama huku akinitazama kwa hasira.

“Nini nitafanya mdogo wangu”

“Nini, nini, wewe ni mtoto kwani?”

“Judy nakuomba twende chumbani, tafadhali nakuomba twende chumbani”

“Ukanisage na mimi si ndio”

“Hapana Judy nakomba tafadhali”

“Nimekuambia mimi na wewe sio ndugu kabisa, na kuanzia hivi kila mtu afe kivyake sawa?”

“Hapana Judy nakuomba nipo chini ya miguu yako”

Sikujali kuna wapambaji wanao tutazama mimi na Judy, nikampigia magoti huku nikimsisitiza kumuomba anisikilize kwa dakika za mwisho.

“Jojo vipi?”

Nilimuona Nuru huku akipandisha kwa kasi kwenye ngazi, akajaribu kunishika mkono ili aninyanyue.

“Niache na wewe”

Nilizungumza kwa hasira huku nikimtazama Nuru usoni mwake. Judy akapandisha ngazi na kuanza kuelekea chumbani tulipo toka huku akimtazama Nuru kwa macho makali sana.

“Jojo ni nini kinacho endelea?”

“Hembu endelea na mambo yako, haya ni matatizo yangu mimi na mdogo wangu wewe hayakuhusu”

Nilimjibu Nuru kwa hasira sana hadi yeye mwenyewe akabaki akiwa ameshikwa na bumbuwazi. Nikamfwata nyuma nyuma Judy hadi ndani ya chumba kilicho andaliwa kwa ajili yake.

“Una dakika tano za kuzungumza, ukishindwa ninaondoka zungu na sahau kabisa kuhusiana na mimi”

Taratibu nikapiga magoti mbele ya Judy, nikaishika miguu yake na kuangua kilio kikali.

“Kulia kwako Jojo hakinisaidi kabisa”

“Miasha yangu hayana thamani yoyote bila kuwa na wewe. Najua kwamba hata marehemu mama hato penda kutuona kwamba mimi na wewe mahusiano yetu yanavunjia kwa namna hii”

“Acha unafki, tena koma kabisa kumtumia marehemu mama katika hili swala sawa”

“Nimekuelewa, ila kuna sababu zilinifanya niweze kukubaliana na hii ndoa”

“Sababu gani?”

“Ni juu ya usalama wa mwanangu. Nuru alisema kwamba nisipo kubalian ana yeye basi anakwenda kumuua mwanangu na kumuua baba wa huyu mtoto ambaye ni Eddy”

“Eddy alitetwa hapa akiwa amepigwa, akiwa hajiwezi na bado nusu atumbukizwe kwenye sisiwa cha mambo, unahisi mimi ningefanya nini lakini jamani”

Judya akaka kimya huku akinitazama.

“Ni bora nimuumize Eddy ili maradi awe salama”

“Hicho unacho kizungumza ni kweli?”

“Ndio ni kweli, maisha yangu hayana amani. Laiti ingekuwa si huu ujauzito basi ningefanya chochote ili mradi kupigania penzi langu kwa Eddy ila sikuweza kufanikisha ndoto zangu na nimejikuta nikiishia kutekwa na nina bahati sana mdogo wangu”

Taratibu Judy akaninyanyua na kunikumbatia.

“Nilazima leo tutoroke dada yangu”

“Kweli?”

“Ndio ni lazima tutoroke”

“Tutatoroka kivipi ikiwa kisiwa hichi kimetawaliwa na ulinzi mkali sana na kwenye maji huko kuna papa wakali sana”

“Usijali nipe muda wa kutafuta ni mbinu gania mbayo inaweza kutusaidia kuweza kutoka humu ndani”

“Sawa”

“Ila siku nyingine unyooshe maelezo ukiwa umefanya kosa sawa”

“Sawa”

“Mimi nipo nje”

Judy alizungumza huku akitupa kipochi chake kitandani, nikakaa kitandani na kujilza chali huku na mimi nikianza kuumiza kichwa juu ya kujua ni jinsi gani ninaweza kutoroka humu ndani. Mlango ukafunguliwa na akaingia Nuru taratibu akaka pambeni yangu.

“Jojo”

“Mmmmm”

“Mdogo wako ana anamatatizo gani?”

“Tutazungumza baadae”

“Sawa, wale watu wa saloon wamesha fika”

“Wapo wapi?”

“Katika lile jumba jengine, wanahitaji waweze kutupima vipimo vya nguo ili waweze kuzishona kwa muda huu”

“Ahaa…..sawa”

Nikanyanyuka na tukatoka chumbani humu na moja kwa moja tukaelekea katika jumba la pili. Tukawakuta wanamitindo wakiwa tayari wamesha jiweka sawa kwa ajili ya kutuhudumia sisi. Wakaanza kutuonyesha picha za magauni ambayo tutapenda tuvae.

“Ila kama dada hapo ungevaa suti hii ya dark blue”

Mwana mitindo huyu anaye tuonyesha hizi picha alizungumza huku akinitazama usoni.

“Na tumbo hili kweli inafaa?”

“Ndio inafaa, na itakupendeza sana, utaonekena kama mwanaume mwenye pesa zake vile”

“Hahaaaa”

“Mimi nipenda hili gauni refu”

Nuru alionyesha gauni refu la harusi.

“Na munayashona ndani ya muda gani?”

“Hili gauni ndani ya lisaa, na hii siti ndani ya dakika thelathini hivi”

“Sawa”

Mwanamitindo huyu akaanza kunipima mimi vipimo vya mwili wangu. Kisha akafwatia Nuru naye katika kupimwa vipimo vya mwili wake kisha baada ya hapo mashono ya nguo zetu yakaanza rasimi. Tukatoka katika chumba hichi na kuingia katika chumba kingine ambacho yupo sonara pamoja na vijana wake. Naye akatuonyesha ni pete za aina gani pamoja na mikufu ya aina ipi tunayo ihitaji ili aanze kututengenezea humu humu ndani.

“Hivi zile pete ambazo unaweza kufahamu mwenza wako yupo wapi si unaweza kuzitengeneza?”

Nuru alizungumza na kunifanya nimtazame usoni mwake kwa mshangao

“Yaaa naweza”

“Tutengenezee hizo”

Nuru alizungumza, sonara huyu kwa haraka akatuonyesha picha ya pete hizo jinsi zinavyo kua, kwa kutumia laptop yake.

“Yaa ewala hizi hizi zitatufaa au unasemaje baby?”

“Sawa mimi sina tatizo”

“Ila furaha mpenzi wangu unaonyesha sura ya huzuni hadi napata wasiwasi”

“Wasiwasi wa nini?”

“Wasiwasi tu mpenzi wangu”

“Usijali mimi na wako tu”

Nilizungumza huku nikimshika shika Nuru kiuno chake. Tukatoka katika chumba hichi na kuingia katika chumba ambacho tukakuta vitu vyote vinavyo patikana katika masaluni mengi hapa vipo. Tukachagua misuko tunayo hitaji kusukwa na zoezi hilo likaanza kufanyika, huku Nuru akipiga hadithi za hapa na pale ili mradi kunifurahisha.

Mimi ndio nikawa wa kwanza kumalizwa katika kuwekwa nywele zangu sawa. Nikaaga na kutoka ndani humu, nikarudi katika jumba jengine, nikakuta na Judy kwenye ngazi za kushuka kwenye gorofa.

“Jojo, Jojo”

Judy aliniita huku akinifwata kwa haraka, akasimama karibu yangu na kuninong’oneza.

“Nimepata mbinu ya kutoroka hapa kisiwani na kama huto jali tuondoke sasa hivi”

Meneno ya Judy yakanifanya nimtazame usoni mwake huku nikiwa nimejawa na mshangao mwingi sana kwani ndio kwanza ni mchana na ulinzi uliopo hapa ni mkali kiasi kwamba sihui hiyo mbinu yake ya kutoroka mchana imekaaje.



“Sasa hivi?”

Niliuliza kwa mshangao huku nikimtazama Judy usoni mwake.

“Ndio tuondoke sasa hivi”

“Tunaondoka na nini?”

“Kuna ndege moja ya mizigo ya wapambaji nimeiona kule uwanjani, baadhi ya wapambaji wanatoa vitu kwenye ndege hiyo. Nimepata nguo zao za wale wabeba mizogo, sasa tunaweza kwenda na kujichanganya humo ndani”

Wazo la Judy ni zuri japo ni la hatari kubwa sana, ila linaweza kufanya kazi na kututoa katika janga hili la mimi kumuoa mwanamke mwenzangu. Nikashusha pumzi usonimwangu huku nikitazama jinsi wapambaji hawa wakiendelea kuzunguka huku na kuhu wakihakikisha kwamba wanafanya mazingira ya eneo hili yanafanya kazi vizuri.

“Hiyo ndogo umejua ioandoka saa ngapi?”

“Sijajua inaondoka saa ngapi, ila nahisi muda si mrefu”

“Ila Ikiwa hatujui inadoka saa ngapi itakuwa ni hatari sana, tusije tukaingia ndani ya ndege na ikazuiwa kuonda na tukachomolewa humo ndani ikawa aibu nyingine hiyo”

“Mmmmm sasa tunafanyaje, ikiwa hiyo ndio nafasi ya pekee ambayo mimi nimeiona inafaa kwa sasa”

“Twende chumbani”

Nilizungumza huku nikipandisha ngazi, Judy akaanza kunifwata nyuma nyuma hadi tukaingia katika chumba chake.

“Tusitoroke leo”

“Kwa nini?”

“Nina maana yangu kubwa sana”

“Ndio hiyo niambie una maana gani?”

“Nuru amesema kwamba endapo nitamuoa, na mwanangu akizaliwa atampatia asilimia sabini na tano ya utajiri wake”

“Na wewe unamuamini mameno yake?”

“Ndio nina muamini”

“Na umedhamiria kabisa kumuoa mwanamke mwenzako?”

“Sina jinsi Judy, najua sasa hivi tukitoroka, lazima atamdhuru Eddazaria ambaye sifahamu kwa sasa yupo wapi?”

Judy akaka kimya huku akionekana kuwaza jambo fulani.

“Laiti kama ningejua kwamba Eddy yupo sehemu salama na ya kueleweka basi ningefanya chochote kutoraka, na hata ndoa yenyewe nimekubaliana kwa maamuzi kwamba Eddy asiuwawe, laiti ningeleta ubishi mama wa watu leo engekuwa analia msiba wa kijana wake.”

“Sasa…..ahkaaa….”

“Najua unaumiza kichwa juu ya hili swala, acha tukubaliane na hili jambo lipite kisha maisha yasonge mbele”

“Ila kusema kweli sijapenda kabisa, huu ni ushetani”

“Natambu hilo mdogo wangu, ila nitafanye na hili tumbo. Nikicheza vibaya naweza kukupoteza hata wewe, kwa maana wanaweza kukutumia wewe kama chambo wa kunishinikiza mimi katika maamuzi hayo.”

Judy akaka pembeni yangu huku akishusha pumzi nyingi sana.

“Na mimi kurudi Tanzania inakuwaje?”

“Ngoja kwa nza hii ndoa ipite, kisha baada ya hapo nitazungumza naye ili uweze kurudi nyumbani, ila ukirudi ninakuomba sana umuangalie Eddy”

“Mmmmmm”

“Una guna nini sasa?”

“Hmana, ila umependeza huko kichwani”

“Asante”

Tukaendelea kuzugungumza mambo mawili matatu ili maradi kulitoa wazo la mimi kuoa kwa siku ya leo. Tukakumbushiana maisha ya utotoni na shida kadhaa ambazo tulizipitia.

“Ina maana huna mpenzi?”

Nilimuuliza Judy mara baada ya kufika katika kipingele cha mahusiano.

“Sina”

Alinijibu huku akitabasamu.

“Apia kwa mwenyezi Mungu?”

“Mambo ya kuapia ya nini tena dada”

“Si huna mpenzi, apia kama ni kweli?”

“Hahaaa, ninaye ila sijampenda kusema kwamba nina mpenda kutoka moyoni mwangu”

“Yeye yupo wapi?”

“Yupo pale pale kwenye kampuni yetu”

“Mmmmm kuwa makini, vijana ambao tuna waajiri sio kama watakuwa wamekupenda wewe kutoka moyoni, ila watauwa wamekutamani”

“Ndio maana nikasema sijampenda kutoka moyoni, yupo kama hayupo vile.”

“Sawa, mimi ngoja nikamilishe hili jambo, najua sasa hivi ni baya ila kwa maisha ya baadae tutakufa matajiri”

“Ni kweli dada”

Mlango ukagongwa wa chumbani mwetu. Judya akaenda kuufungua, akaingia Nuru huku akiwa amebeba gauni lake pamoja na suti yangu.

“Baby tayari hembu jaribisha suti yako”

Nuru alizungumza huku akinikabidhi suti yangu, nikaichukua na kitazama vizuri. Nikavua dera langu kisha nikaivaa suti hii.

“Best umependeza”

Judy alizungumza huku akiwa amejawa na furaha sana kana kwamba amesha sahau ubishi wake wote alio kuwa akinifanyia juu ya ndoa hii.

“Umeona wifi”

“Yaa amependeza sana”

“Musiseme tu nimependeza, ikiwa Nuru wewe hujavaa”

“Hili la kwangu yaani nikilivaa, kulivua ni kazi kweli kweli”

“Kwani umelijaribisha?”

“Nasubiria muda ufike nilivae. Pete atazileta yule sonara mkuu baadae kidogo”

“Sawa”

“Kwenye ndoa kama zenu hivi hakuna wasimamizi”

Judy aliuliza huku akitutazama usoni mwetu.

“Kwa mimi sifahamu?”

“Wapo, alafu nilikuwa nimelisahau hilo.”

“Mimi nitamsimamia dada yangu”

“Kweli?”

Nuru aliuliza kwa shauku kubwa sana.

“Ndio nitamsimamia dada yangu”

“Sawa mimi ngoja nikamtafute wa kunisamimia”

Nuru akatoka ndani humu akiwa amejawa na furaha sana.

“Wewe. Si ulikuwa hutaki hili swala?”

“Tunampumbaza, najua nini namaanisha”

Nikatingisha kichwa nikiashiria kwamba nimemuelewa Judy. Masaa yakazidi kwenda kasi na wageni kutoka meneo mbali wakazidi kumiminika. Wadada wawili wa saluni wakaingia kwenye chumba chetu na kuanza kutupamba mimi na Judy. Majira ya saa moja na nusu tukawa tayari tumesha maliza kujiandaa. Tukatoka chumbani humu huku tukimfwata mtu maalumu aliye pewa jukumu la kutupeleka ukumbini.

“Mapigo ya moyo yananienda mbio kama nini?”

Judy alizungumza huku akiwa amenishika mkono wangu wa kulia.

“Unaogopa nini?”

“Yaani hata sijui”

“Jikaze bwana”

“Mmmm unajua hivi tunavyo fanya ni vituko?”

“Hahaaa vituko gani?”

“Mmmmm yaani hatari kweli kweli”

Tukafika nje ya eneo ambalo tumeandaliwa kwa ajili ya kuingia ukumbini. Watu wenye pesa zao na walio valia vizuri wameudhuria harusi hii.

“Munaweza kuingia sasa”

Mtu huyu aliye kuwa anatuongoza alituambia huku yeye akiwa amesimama mlangoni. Mziki wa kinanda unao pigwa taratibu ukaanza kusikika vizuri masikioni mwatu. Taratibu tukaanza kutembea kwa mwendo wa taratibu, kuingia katika ukumbi huu. Watu wengi wenye simu zao zenye kamera hawakusita kutupiga picha huku wengine wakiturekodi video.

‘Ehheee Mungu nisamehee, umasikini kwa kweli ni mbaya’

Nilizungumza kimoyo moyo huku tukizidi kusonga mbele. Kila hatua ninayo zidi kusonge mbele ndivyo jinsi ninavyo jitahidi kuweka tabasamu langu vizuri. Nikaanza kupunga mkono taratibu, jambo lililo wafanya watu wote humu ndani kuzidisha shangwe za kunishangilia kwa makofi. Tukafika sehemu ya mbele kabis ya ukumbi huu ambapo yupo padri. Padri kwa ishara akatuonyesha sehemua mbayo tunapaswa kusimama.

“Kumbe watu wamekuja wengi hivi eheee?”

Judy alininong’oneza.

“Ndio wamekuja wengi sana”

“Mmmm nilijua watakuwa watu wawili watatu”

“Wewe si uliona jinsi watu walivyo kuwa wanatiririka”

“Kweli aisee”

Mziki ukabadilila na mpiga kinanda akapiga kwa mtindo mwingine. Tukageuka nyuma na kumuona Nuru anavyo ingia ukumbini humu, huku gauni alilo livaa likiwa ni refu sana na linaburuzika chini. Pembeni yake yupo dada mmoja mrefu na mwenye asili ya kizungu. Kwa mwendo wa taratibu wakatembea hadi hapa tulipo simama sisi. Taratibu nikamsogelea Nuru na kumvua kitambaa kilicho funika uso wake, kisha taratibu nikambusu mdomoni mwake na tukasimama vizuri na kumtazama padri huyu.

“Umependeza baby”

Nilimsifia Nuru kwa sauti ya chini ambayo hata Padri aliye simama mbele yetu hakuweza kuisikia.

“Asante mpenzi”

Padri akaanza kuongoza misa hii ambayo kusema kweli sidhani kama kidini inaeleweka, kwani baadhi ya watu wanakunywa mvinyo kama vile hakuna misa yoyote. Ikafika hatua ya kula kiapo cha kuwa na Nuru katika shida na raha, kisha nikamvisha pete kidoleni mwake. Ikafika hatua zamu yangu, na yeye Nuru akala kiapo cha kuwa nami kwenye shida na raha, kisha akanivisha pete. Padri akaturuhusu tuweze kupena denda zito. Nuru akashika nyuma ya shingo yangu kwa mkono wake wa kulia na tukaanza kunyonyana midomo yetu. Watu wakazidi kushangilia na kufurahi sana kwa kitendo hichi ambacho kwa namna moja si kizuri mbele ya mwenyezi Mungu, ila kwa hawa binadamu ni sawa tu.

“Nakupenda sana Jojo wangu”

“Nakupenda pia Nuru”

Tukauongoza hadi katika sehemu ya kukaa, kisha ukumbi ukafanyiwa marekebisho ya haraka haraka na wapambaji, walio jipanga kisaswa sawa kuhakikisha yale mandhari ya kikanisa yanaondolewa na yanabaki mandhari ya kushangweka.

“Mumependezana kwa kweli”

Judy alizungumza huku akiwa amejawa na tabasamu pana usoni mwake.

“Kweli?”

“Ndio, yaani mume endana”

“Asante wifi”

“Sasa inabidi umtunze dada yangu si unaona hali yake hiyo ilivyo”

“Usijali wifi nitaifanya hiyo kazi kwa asilimia mia moja wala sinto kuangusha”

“Siku nirudi Tanzania alafu huku nyuma nije kusikia kwamba ulikuwa unamtesa dada yangu aisee, sijui nitakufanyaje wifi”

Judy alizungumza kiutani utani ili mradi tu kutufurahisha.

“Usijali, hato jutia kwa kuwa na mimi”

“Sawa kama hato jutia kuwa na wewe”

Muongoza sherehe akatuomba tuweze kukaa mbele ya ukumbi huo kwenye sofa nzuri za garama zilizo andaliwa dakika chache zilizo pita. Sherehe ikaanza rasmi huku wageni rasmi wakitoa zawadi nyingi sana. Katika maisha yangu leo ndipo nimeshuhudia jinsi watu walivyo na jeuri ya pesa, kwani pesa nyingi za kimarekani, zimemwaga na baadhi ya wageni rasmi kwenye eneo tulilo kaa wakitupongeza kwa hatua nzuri tuliyo fikia ya kuoana.

“Natamani hata niziokote”

Judy alininong’oneza na kunifanya nicheke sana. Watu maalumu walio pangwa katika kupokea zawadi zetu wakakusanya pesa hizi na kuziweka kwenye mabigi kama sita hivi makubwa na yakajaa vizuri tu.

“Hawa ni wafanya biashara wezangu ambao nilikuwa ninashirikiana nao kwenye mambo mengi sana”

Nuru alizungumza huku akiwa amejawa na tabasamu.

“Ahaa sawa sawa”

Wakati wa chakula ukawadia. Tukaelekea kwenye meza ya kupatia chuakula, tukachukua chakula chetu na kurudi tulipo kuwa tumekaa, taratibu tukaanza kula huku stori ha hapa na pale zikiendelea.

“Judy maliza kula unipeleke haja ndogo”

Nilizungumza mara baada ya kumaliza kula.

“Sawa”

“Ngoja nikuepele tu mimi”

“Hapana mpenzi wangu, hawa watu hatuwezi kuwaacha watu hao peke yao humu ukumbini ikiwa wamekuja kwa ajili ya sherehe yetu”

“Ahaa sawa”

“Twende zetu”

Judy alizungumza huku akijifuta mikono yake kwa kutumia karatasi laini, nikambusu Nuru kwenye lipsi zake kisha nikanyanyuka na kutoka humu ndani ya ukumbi, tukaingia kwenye vyoo maalumu vilivyo andaliwa kwa ajili ya wageni waalikwa. Nikaingia ndani ya choo maalumu na nikajisaidia haja yangu, kisha baada ya hapo nikatoka na kumkuta Judy akiwa hayupo humu ndani zaidi ya mwana mama mmoja mwenye nywele ndefu sana hadi mgongoni. Mwana mama huyu akavua miwani yake na kwenye zake kadhaa zilizo kuwa zimefunika uso wake akazirudisha nyuma, nikajikuta nikistuka sana.

“Hongera”

Mama mkwe alizungumza huku akinitazama usoni mwangu kwa macho makali sana yaliyo nifanya niaze kutetemeka mwili wangu wote na nikakosa hata cha kumjibu.



Mama mkwe akaanza kunisogelea, jambo lililo nifanya nianze kurudi nyuma nyuma huku nikizidi kuogopa kwa kweli kwani sikutarajia wala kukutana naye katika hili.

“Mwanangu amejitoa maisha yake kwa ajili yako, amepigana kwa ajili yako. Ila haya ndio malipo uliyo kusudia kumlipa si ndio?”

Nilijibu huku nikitingisha kichwa changu, machozi yakaanza kunimwagika usoni mwangu. Kurudi kwangu nyuma kote nikajikuta nikiwa nimefika ukutani na kushindwa kurudi nyuma zaidi ya hapa.

“Ulikosa nini kwa mwanangu?”

Mama mkwe alizungumza huku machozi yakimlenga lenga usoni mwake.

“Mama…..”

“Koma mimi sio mama yako tena. Nilikupenda, nilikujai zaidi ya hata binti yangu, nilikuwekea walinzi wa kutosha ili mradi uwe salama, ila ukatoroka nyumbani, ukawapiga walinzi na ukaja huku kuolewa na huyu shetani ambaye siku zote ulitudanganya kwamba ni adui yako ila sasa hivi ni mkeo si ndio?”

Nikakosa cha kumjibu mama mkwe zaidi ya kuangua kilio kilicho mfanya mama mkwe kwa haraka kuniziba mdomo wangu.

“Shiiii…..sitaki unafiki mimi, nipo hapa kwa ajili ya jambo moja tu. Ninamhuhitaji mjukuu wangu”

Macho yakanitoka mara baada ya kusikia kauli hiyo ambayo inazidi kuniogopesa.

“Najua una miezi michache kabla ya mjukuu wangu hajazaliwa, akizaliwa tu si wa kwako, la sivyo utanitambua mimi ni nani. Umenielewa?”

Nikatingisha kichwa nikimuashiria mama mkwe kwamba nimemuelewa. Taratibu mama mkwe akaniachia mdomo wangu, kisha akaziweka nywele zake kama alivyo kuwa ameziweka na kutoka humu ndani, nikajikuta nikikaa chini bila kupenda. Baada ya dakika kama mbili Judy akaingia huku akiwa ametabasamu, alipo niona nimekaa chini huku ninalia kidogo sura yake ikabadilika na kuonekana kama ni mtu mwenye mawazo kidogo.

“Weee Jojo vipi mbona umekaa chini?”

Judy aliniuliza huku akichuchumaa mbele yangu.

“Mama”

“Mama, mama kafanyaje?”

“Amekuja”

“Hahaaaa……umechanganyikiwa rafiki yangu?”

“Nichanganyikiwe na nini na wewe, nimekuambia mama mkwe amekuja hapa unasema nimechanganyikiwa kwanza ulikuwa wapi?”

Niliongea kwa kufoka huku nikimtazama Judy usoni mwake.

“Mama mkwe amekuja hapa, kivipi na saa ngapi, ikiwa mimi nilikuwa hapo nje nikipipa piga story na jamaa mmoja hivi”

Nikamtazama Judy kwa hasira, naamini atakuwa anatambua uwepo wa mama mkwe hamu ndani.

‘Siwezi kupokonywa mwanangu ikiwa nimembeba mimi mwenyewe’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikijitahidi kunyanyuka, Judy akanisaidia, nikajiweka sawa nguo yangu.

“Niambie mama mkwe ameingiaje humu ndani?”

“Ameingia humu ndani na amenipa onyo kali sana na anataka nikijifungua tu mtoto amchukue anasema kwamba huyo mtoto hato kuwa wangu tena”

“Heee….jamani mbona kila siku shida tu. Haki ya Mungu nimekaa hapo nje na sijamuona mtu akiingia humu wala kutoka humu ndani”

“Kwa ajili ya mwangu, nimehidi kufanya chochote ili mradi mwanangu awe hai”

Nilizungumza kwa msisitizo huku nikimtazama Judy usoni mwake, nikajifuta mashavu yangu na kuyaweka sawa ili michirizi ya machozi isonekane. Nilipo hakikisha kwamba nipo vizuri, tukatoka chooni humu. Tukakutana na walinzi wanne wa Nuru wakiwa wamesimama nje ya choo hichi wakionekana kwamba walikuwa wakitusubiria, wakatusindikiza hadi nje ya mlango wa kuingilia ukumbini. Tukaingia na Judy na moja kwa moja tukelekea katika sehemu tulizo kuwa tumekaa.

“Baby vipi mbona umechelewa?”

Nuru aliniuliza kwa sauti ya kuninong’oneza. Nikajifikiria kwa muda kidogo kisha nikamsogelea na kumnong’oneza.

“Umemualika mama Eddy?”

“Mama Eddy…..!!! Hapana”

“Imekuwaje amekuja huku kwenye sherehe yetu?”

Nilimuuliza Nuru kwa ukali, kwa mana hapa hakuna jinsi zaidi ya kuhakikisha vita niliyo ianzisha juu ya kumlinda mwanangu aliyopo tumboni mwangu ninaishinda na sinto hitaji mtu wa aina yoyote aweze kunipokonya mwanangu huyu.

“A..haa…hapana sijafahamu kwa nini yupo humu ndani!!”

Nuru alinijibu huku akiendelea kupepesa pepesa macho yake huku na kule.

“Kwa nini vijana wako hawaimarishi ulinzi nataka akamatwe sasa hivi”

“Sawa mpenzi”

Nuru kwa ishara akamuita mmoja wa walinzi wake walio ndani ya huu ukumbi, akamnong’oneza.

“Amevaa nguo gani?”

Nuru aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.

“Amevaa gauni la silva na lina vimetometo, ni refu kuanzia juu hadi chini”

“Umesikia”

“Ndio mkuu”

“Hakikisheni kwamba mama huyo anakamatwa haraka iwezekanavyo”

“Pia amevaa miwani nyeusi pamoja na nywele zake amezielekezea mbele hivi”

“Nimekuelewa madam”

“Yaani sherehe hii ikiisha ninahitaji kumuona huyo mama akiwa mikononi mwane sawa?”

Nilizidi kuzungumza kwa ukali ulio mfanya hadi Judy kunifinya kidogo kwa maana nimejisahau kabisa kwamba nipo mbele za watu. Mlinzi huyu akaondoka, na kunifanya nianze kufikiria fikiria ni adhabu gani nitampatia mama mkwe pale atakapo kamatwa mikononi mwangu.

“Mbona umekasirika kuna nini?”

Judy aliniuliza huku na yeye akininong’oneza kwa upande wake.

“Nahitji mama mkwe akamatwe”

“Akamatwe….!!!?”

“Ndio”

“Weee Jojo, umekuwaje, mama wa watu kuna kosa gani ambalo amelifanya jamani?”

“Nimesha sema hakuna mtu wa kubadilisha maamuzi yangu, hujui maumivu ya mtoto wewe, shika mimba uone jinsi maumivu yake jinsi yalivyo.”

Judy akaka kimya huku akishusha pumzi nyingi. Hata furaha ya sherehe hii siipati tena, akilini mwangu ninawaza ni jinsi gani nitakavyo muadhibu mama mkwe. Nikiwa katika dimbwi la mawazo gafla tukaanza kusikia kelele za watu walio kaa nyuma ya ukumbi, jambo hili kidogo likatushangaza sana. Moshi mwini na mzito ukazidi kutawala ndani ya ukumbi huu, na moshi huu ukaanza kumpalia kila mtu humu ndani huku machoni machozi mengi yakianza kutububujika. Walinzi wa Nuru kwa haraka wakatushika na kuanza kututoa humu ndani ya ukumbi huu huku wakitupa vifaa maalumu vya kuzuia moshi huu, usiendelee kutupalia.

Nje huku tulipo toka napo moshi huu umetawala sana kiasi kwamba tumejikuta tukizidi kuchanganyikiwa kwani mbele tunapo kwenda hatupaoni na hata nyuma tunapo toka napo pia hatupaoni. Nikastukia kishindo kizito pembeni yangu, mlinzi aliye kuwa amenishika mkono akijitahidi kuhakikisha kwamba ananitoa kwenye janga hili, nikamuoa akiwa amelala chini. Gafla kitu chenye ncha kali kikanichoma kwenye paja langu, nikajitahidi kupiga hatua moja mbele ila nikajikuta miguu na mwili mzima ukiwa mzito na taratibu nikajikuta nikianguka chini na hata kabla sijafumba macho, yangu nikahisi nikishikwa mikono yangu miwili na kunyanyuliwa juu juu, kadri muda na dakika zinavyo zidi kwenda ndivyo jinsi nilivyo jikuta mwili mzima ukiishiwa nguvu na nikajikuta nikilala fofofo.

***

Taratibu nikafumbua macho yangu huku yakiwa yamejawa na ukungu mwingi sana machoni mwangu. Kadri mud aulivyo zidi kwenda ndivyo jinsi macho yangu yalivyo zidi kupata nguvu ya kuweza kuona eneo hili ambalo ni kama chumba ambapo humu ndani kuna walinzi wawili walio zifunika sura zao na vinyago vilivyo waacha macho tu, huku kila mmoja akiwa ameshika bunduki aina ya AK47. Nikajaribu kunyanyuka kwa ngvu ila nikashindwa, kwani mikono yangu imefungwa na kamba nguvu na jinsi nilivyo chanuliwa hii mikono yangu, ni kama jinsi Yesu alivyo sulubishwa msalabani.

“Nipo wapi nyinyi nguruwe”

Nilizungumza kwa kufoka huku nikijaribu kujitahidi kuitoa mikono yangu ila sina nguvu ya kukata kamba hizi aina ya manila. Nikaendelea kulala hapa kitandani nilipo funga pasipo kusemeshwa chochote na hawa watu. Baada ya kama nusu saa, mlango ukafunguliwa akaingia mama mkwe huku akiwa ameongozana na mzee mmoja wa kihidi aliye valia koti jeupe. Kwa kumtazama tu huyu mzee unaweza kufahamu kwamba ni daktari.

Mama mkwe akanitazama kwa macho makali yaliyo jaa chuki na hasira dhidi yangu. Daktaria akanifunua tumbo langu.

“Unataka kufanya nini?”

Nilizungumza kwa hasira huku nikijitahidi kurusha rusha miguu yangu huku na kule nilimzuia daktari huyu kuto kufanya jambo lolote kwangu. Mama mkwe kwa ishara akawaambia vijana hao wanao nilinda kunifunga miguu yangu. Kijana mmoja akatoa kamba iliyo kunjwa vizuri, akaifungua, akanishika mguu wangu wa kulia akaufunga kwa kamba, pamoja na kitanda, kisha akashika mguu wangu wa kushoto nao pia akaufunga na kusema kweli sina ujanja wa kuweza kufanya chochote.

Daktari akaanza kulishika shika kidogo tumbo langu, akachukua kifaa maalumu ambacho kinatumiwa na madaktari katika kusikilizia mapigo ya moyo. Akaniweka kifuani mwangu upande wa mapigo ya moyo. Alipo maliza zoezi hilo akamsimama na kumtazama mama mkwe.

“Mtoto anaendelea vizuri”

“Ndani ya muda gani tunaweza kumtoa akiwa hai?”

Nikajikuta nikistuka na kumtolea macho mama mkwe, kwani kauli yake ni nzito hususani katika kipindi kama hichi.

“Mmmm kama baada wa wiki mbili, anaweza kuwa katika mzunguko mzuri?”

“Wiki mbili?”

“Ndio mkuu”

“Sawa unaweza kwenda”

Daktari huyu akatoka chumbani humu na kuniacha mimi na mama mkwe pamoja na walinzi wake hawa wawili.

“Jojo nahisi umenisahau au kwa lugha nyepesi niseme kwamba umeshauo kanuni nilizo weza kukupatia kipindi ulipo kuwa unakuja kutambulishwa kwangu si ndio?”

Mama mkwe alizungumza huku akikaa pembeni yangu, sikumjibu kitu chochote zaidi ya kumtazama kwa macho ya hasira.

“Unajua ni kwa nini kwa mara ya kwanza nilikushukia bastola mara tu ya kuja nyumbani kwangu siku ile asubuhi tulipo kuwa tunafanya mazoezi?”

Nikatingisha kichwa huku machozi yakinilenga lenga usoni mwangu.

“Moja, niliweza kufahamu kwamba kuna mambo kama haya yanaweza kuja kutokea na kweli yametokea. Mbili niliweza kufahamu harakati zako za kushuhulika na madawa ya kulevya, toka ukiwa nchini China na kurudi Tanzania”

Mama mkwe alizungumza kwa msisitizo ulio nifanya niwe mnyonge sana.

“Niliweza kukupa muda mzuri tu wa kuweza kujirekebisha kwa maana mwanangu alikupenda, ila si wewe hukumpenda mwanangu.”

“Ulimtumia kama daraja la kufanikisha safari yako ya usanii wa kuigiza. Leo yapo wapi, leo hii umerudi kwenye maisha yako ya ushatani na kudhihirishia dunia kwamba wewe ni msagaji kabisa si ndio?”

“Mimi sina ugomvi na mtu yoyote kwa sasa, si wewe ila ninacho angalia ni kizazi changu, sihitaji kizazi changu kiteseke tena nikiwa bado nipo hai kwenye huu ulimwengu”

“Hicho kilichopo tumboni mwako ni kizazi chungu, ni mjukuu wangu kama ilivyo kuwa kwa kina Gody wote, sasa siwezi kuona mjukuu wangu anakwenda kuishi na mama ambaye hajulikani ni binadamu au shetani kwa tabia zake mbovu”

Mama mkwe alizidi kuzungumza maneno yaliyo zidi kunigopesa kwa kweli, machozi yakazidi kunitoka.

“Una wiki mbili mimba yako itemize miezi saba. Kama huyo Eddy nilimzaa na miezi saba tu, basi huyo mjuu kuu wangu utakwenda kumzaa kwa miezi saba sawa”

“Mama…..”

“Mimi sio mama yako. Ni binadamu gani ambaye wanangu wanajitoa maisha yao sadaka kwa ajili yako. Mimi mwenyewe najaribu kutumia pesa yangu kuhakikisha kwamba ninakuwekea ulinzi, ninakutunza kana kwamba mtoto wa malkia, ila hujali hilo zaidi unaendelea kufanya mambo ya kipuuzi.”

“Hapana mama nipo tayari kukukabidhi mtoto akiwa amezaliwa, nakuomba sana mama yangu uweze kunisamehe katika hili, nakuomba usimtoe mwanangu akiwa na miaka saba”

Nilizungumza kwa ujasiri pasipo kujali kama mama mkwe atafurahi au atachukia. Kabla mama mkwe hajanijibu chochochote simu yake ikaita akaitoa katika mfuko wak, akaitazama kwa muda, nikaona ni whatsapp video call, akaipokea na kuiweka simu yake mbele kidogo ili aweze kumuona mtu huyo aliye mpigia. Sote tukamuona Nuru akiwa ndio aliye piga simu hiyo, Nuru akatazamana na mama mkwe kwa sekunde kadhaa huku Nuru nikiomuona jinsi alivyo fura na hasira. Nuru akaisogeza kamera ya simu yake pembeni na tukamuona Eddazaria akiwa ameshikiliwa na ile mibaunsa iliyo kuwa imemteka, kisha akairudisha kamera hiyo usoni mwake.

“Mwanao Eddy na mume wangu Jojo, tufanye mabadilishano ndani ya msaa matatu kuanzia hivi sasa, tumeelewana?”

Nuru alizungumza kwa jazba kubwa sana huku akimtazama mama mkwe ambaye yupo kimya na hajajibu kitu chochote zaidi ya kunigeukia na kunitazama kwa macho makali sana.



Mama mkwe akakata simu hii kisha akatoka chumbani humu kwa hatua za haraka sana. Zilizo nifanya nikae kimya na maswali mengi yakazidi kunitawala kichwani mwangu, na kujiuliza ni hatua gani ambazo mama mkwe anakwenda kuzichukua. Nikaendelea kukaa katika hali hii ya kufungwa kamba miguuni na mikononi mwangu kwa masaa kama sita hivi, na nilivyo jichunguza kwenye mkono wangu wa kushoto nikakuta pete yangu haipo.

Mlango ukafunguliwa na wakaingia wanawake wawili walio valia suti nyeusi, wakanifungua kamba za mikononi mwangu na knishusha kitandani.

“Vaa hii?”

Mwanamke mmoja alizungumza huku akinikabidhi jaketi la kuzuia risasi(bullet proof). Nikalitazama kwa muda, na akilini mwangu moja kwa moja nikagundua kwamba sasa ni muda wa kwenda kubadilishana kati yangu mimi na Eddazaria ambaye hapo awali nilijua kwamba Nuru atakuwa amemuachia kama nilivyo kuwa nimehitaji aweze kufanya hivyo.

Taratibu nikavaa jaketi hili la kuzuia risasi, tukiongozana na vijana ambao walikuwa wananilinda muda wote ndani ya chumba hichi, tukatika nje na kuwakuta walinzi wengine sita sebleni kila mmoja akiwa amevalia jaketi la kuzuia risasi na kila mmoja wao ana bunduki mkononi.

“Tayari”

Mama mkwe alitoka katika chumba kingine, walinzi wawili wakamfwata, na kuingia naye ndani ya chumba hicho, baada ya muda akatoka akiwa yupo na msichana mwengine ambaye ananishangaza sana, kwani anafanana na mimi kwa kila kitu, yaani hadi ujauzito wangu. Mama mkwe akanitazama mimi kwa muda, kisha akatabasamu na kuanza kutembea kwa hatua za taratibu hadi hapa nilipo simama.

“Huyo mshenzi mwenzio ameamua kulete fujo kwenye familia yanu na ameichafua amani ya familia yangu na mimi ninakwenda kuchafua kila kitu anacho kuhisi kwake kitampa furaha na amani. Sijui unanielewa ni nini ninacho kizungumza?”

Nikakaa kimya na kukosa hata ujasiri wa kumjibu mama mkwe, kwani kwa mbinu hii ya mama mkwe kumtengeneza Jojo wa pili kusema kweli kumenifanya nikate tamaa kabisa ya matumaini yangu kwamba nitajifungau mwanangu akiwa na miezi tisa.

“Kabla sijasahau kitu, nikimrudisha mwanangu mikononi mwangu, sahau juu ya mahusiano yenu na wala usijaribu kumshawishi kwa aina yoyote ile ya kuhitaji kurudiana naye. Sijui umenielewa”

“Ndio mama”

“Mimi sio mama yako”

“Sawa nimekuelewa”

Nilijibu huku machozi yakinilenge lenga, kama binadamu ambaye nilisha mzoea huyu mama kumuia mama na niliweza kufanya naye mambo mengi kwa kipindi nilicho ishi naye ni jambo ambalo kusema kweli linaniumiza sana moyo wangu. Nikajikuta nikianza kujilaani ni kwa nini nilishindwa kuweza kusimamia msimamo wangu wa kupigania penzi langu, hata kama mwanangu angeudhurika ila ningeweza hata kuishi katika amani kubwa na Eddazaria na tungemuomba Mungu tungefanikiwa kumpata mtoto mwengine.

Taratibu niajikuta nikipiga magoti chini huku nikizidi kulia kwa uchungu, nikamshika mama mkwe mguu wake wa kushoto, jambo lililo wafanya walinzi wote ndani ya seble hii kubwa kunishangaa sana.

“Mama najua mimi ni mkosefu, najua nimeweze kulete matatizo makubwa kwenye familia yako, ila ninakuomba mama yangu unisamehe. Ninakuomba usinitenganishe mbali na Eddazaria, nakuomba usimfanye kitu kibaya mjukuu wako aliyopo tumboni mwangu, nakuomba nijifungue kwa miezi tisa na uishi naye”

Nilizungumza huku matone ya machozi yangu yakimwagika katuka mguu wa mama mkwe.

“Mimi ni yatima mama, sina ndugu zaidi ya Judy na mwanao kwangu alikuwa ni baba, kwangu alikuwa ni rafiki, kwangu alikuwa ni mpenzi, kwangu atakuwa baba wa mwanangu, kwangu alikuwa mshauri. Tafadhali mama yangu ninakuomba sana, tena sana, unisamehe. Nipo tayari kufa, nipo tayari kwa adhabu yoyote utakayo nipa ila ninakuomba tena moyo wako uridhie kunirudisha katika familia yako”

Mama mkwe akatoa simu yake mfukoni, baada ya sekunde kama tano hivi, nikaanza kuisikia sauti yangu niliyo kuwa ninazungumza na Nuru nikimuamuru ahakikishe walinzi wake wanamakata mama mkwe na nilizungumza kwa kudhamiria kabisa na kutoka moyoni mwangu. Mama mkwe akachuchumaa taratibu na kuingiza mkono wake katika mfuko wa upande wa kushoto wa suruali yangu nakutoa kifaa kidogo sana ambacho kinatumia kunasa mawasiliano ya sauti.

“Jana usiku nilikuwekea hichi kwenye mfuko wa surualia yako pasipo wewe kuweza kufahamu, ili niweze kusikia kila kitu unacho kizungumza.”

“Jana sikuwa na mpango wa kukuteka, na wala sikua na wazo hilo na nilikuja kushuhudia kwa macho yangu kama ni kweli unaolewa tena na mwanamke mwenzako. Na ni kweli, ila haya mazungumzo yako ndio yalinifanya nifanye hivi ili ujue, unapo waza wewe, sisi tulisha pita siku nyingi sana.”

Mama mkwe alizungumza kwa msisitizo ulio zidi kunikatisha tamaa ya kuona sina tena nafasi ya kuwepo katika familia hii ambayo ilinipenda, iliniheshimu hata pale walipo kuja kugundua kwamba mimi ni msagaji, ila bado mama mkwe na wifi yangu waliendelea kuniheshimu, kunijali na haikuwahi siku hata moja, walio tumia udhaifu wangu kuninyanyasa wala kunitenga.

“Kama ulihitaji kunidhuru, basi tambua kwamba sina imani kabisa na wewe. Jojo sikuamini, na wala sihitaji uumize moyo wa mwanangu tena, japo najua anakupenda, ila mapenzi yenu nikiwa mimi kama mama yake. Nikutaarifu kwamba yamesha fika mwisho hata kabla ya nyinyi kuamua kwamba yafike mwisho. Mnyanyueni”

Mama mkwe aliwaambia walinzi wake huku akiutoa mguu wake nilio kuwa nimeushika. Wakaninyanyua, na tukaanza kutoka nje ya hili eneo ambalo kidogo lipo msituni. Nikaona gar inane aina ya Range rover sport, zote zina rangi nyeusi na zote zina fanana. Nikaingizwa kwenye moja ya gari huku Jojo mwengine naye akiingizwa kwenye gari jengine. Mama mkwe akaingia kwenye gari nililo panda na nikaka naye katika siti ya nyuma.

Magari manne ya kwanza ambayo moja wapo yumo Jojo feki, yakaanza kuondoka na kupita njia nyingine, magari mengine manne tuliyopo sisi takapita njia nyingine. Nikatamani sana kuuliza ni wapi tunapo kwenda, ila nikashindwa kutoka nimesha tibua hali ya hewa.

Mama mkwe akaitoa simu yake mfukoni na kuanza kuiminya minya taratibu, kisha akaiweka sikioni mwake.

“Ehee”

“Hakikisheni kwamba yeye na kundi lake hakuna hata mmoja anaye ondoka hai”

“Ndio sisi tutawaangalia kwa umakini sana na endapo msaada utahitajika basi tutakuwa nyuma yenu”

“Hakikisheni kwamba nyote munatoka salama”

“Sawa”

Mama mkwe mara baada ya kumaliza kuzungumza na mimi akairudisha simu yake mfukoni mwake. Safari hii ikazisi kusonge mbele huku ikiwa ni pori kwa pori, kusema kweli sijui kama bado nipo nchini Dubai au nchi tofauti na Dubai.

“Mama”

Nikajikaza kumuita mama mkwe, akanigeukia pasipo kuitikia kumuita kwangu.

“Natambua ya kwamba mimi ni mkosefu, ila nakuomba mama yangu uweze kunisamehe”

Mama mkwe hakunijubu chochote zaidi ya kuendelea kunitazama usoni mwangu.

“Najua nimembea mjukuu wako, ila sitamani mjukuu wako aje kukutana na maisha kama haya ambayo mimi niliishi, nilizaliwa masikini, katika harakati za maisha yangu, na kufungwa jela nchini China, kulipeleka kuianzisha tabia hii. Tabia ambayo sikufahamu kwamba inaweza kuja kuwa sugu kwenye maisha yangu na kudhuru hata furaha yangu ambayo siku zote niliamini kwamba inajengwa kwa kuwa na pesa nyingi ila sivyo mama yangu.”

“Najua kwamba si wewe wala Eddy ambao munaweza kunipenda tena. Kwa maana Eddy tayari nilisha muacha. Ila mama nilifanya hivyo si kwa kupenda. Nilifanya hivyo kutokana na kuyaokoa maisha ya mwanao. Sikuhitaji kumuona Eddy anakufa, ndio maana niliamua kumuacha mbele ya Nuru ili maradi leo hii awe hai.”

“Niakuaminije?”

“Siku mbili kabla ya hii siku, Eddy aliletwa kule nyumbani kwa Nuru akiwa amepigigwa sana. Alining’inizwa kwenye kisima cha mamba huku akiwa amefunikwa uso mzima na wala sikuweza kufahamu kama ni yeye.”

Nilizungumwa kwa upole na sauti iliyo jaa ushawishi, kwani hii ndio nafasi yangu ya pekee kuhakikisha kwamba niurudisha moyo wa mama mkwe kwenye mstari ulio nyooka, na nikifanikiwa kwa mama mkwe nina imani kwamba kwa Eddy haito kuwa jambo gumu sana.

“Alipo funiliwa kinyago alicho kuwa amefunikwa usoni mwake ndipo nilio weza kufahamu kwamba ni Eddy. Niliambiwa nichague kati ya kumuoa Nuru au Eddy aliwe na mambya. Ningefanya nini mama yangu, ningemuacha Eddy afe ikiwa nina mpenda, eheee?”

Nilizungumza huku machozi yakinimwagika usoni mwangu, mama mkwe akakaa kimywa kwa muda huku akinitazama usoni mwangu.

“Mama sikufanya kwa maamuzi yangu, nilichanganyikiwa mama yangu, na huu ujauzito sikuwa na namna ya kufanya, siwezi hata kurusha teke. Nitafanyeje, niliamua kuokoa maisha ya baba wa mtoto na mwanangu. Japo ni maamuzi magumu kwangu”

Nikaanza kumuona mama mkwe machozi yakianza kumlenga lenga usoni mwake. Akajifuta na kutazama pembeni dirishani.

“Mama kuna mambo mengi sana yametokea hapa, kusema kweli siwezi kumuona Eddy akifa. Ni bora nilipe mimi kwa kufa, kwa maana mimi ndio mkosefu, mimi ndio niliye msabishia matatizo kwenye maisha yake. Na ile kauli ya kusema kwamba nilimpenda ili nimtumie kwenye kazi zangu za uandishi, haipo sahihi mama yangu. Ninampenda, ninampenda sana Eddy. Elewa hilo mama yangu, ninampenda sana mwanao”

Nilizungumza kwa uchungu huku nikimtazama mama mkwe usoni mwake. Mama mkwe akazidi kumwagikwa na machozi pasipo kujibu chochote.

“Eddy ndio mwanaume wangu wa kwanza kunivunja bikra yangu, na sikuwahi kuwa na mwanaume mwengine tofauti yake hadi hapa nilipo fika”

Mama mkwe akanigeukia huku akinitazama usoni mwangu kwa mshangao mkubwa sana.

“Ndio mama Eddy ndio aliutoa usichana wangu, na mteso yote niliyo pitia, mikiki mikiki yote niliyo wahi kupitia, ila yeye ndio aliye weza kunitoa usichana wangu”

Niliongea kwa msisitizo huku nikiendelea kulia. Mama mkwe akatoa simu yake mfukoni na kuanza kuminya minya kisha akaiweka sikioni mwake.

“John”

  ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

BLOG