Search This Blog

Wednesday, November 18, 2020

AISIIIII.....U KILL ME SEASON 2 SEHEMU YA 3/10

 

 

AISIIIII.....U KILL ME SEASON 2 

WRITER…………………………………………EDDAZARIA G.MSULWA
WEBSITE………………………………………… www.storyzaeddytz.com
CONTACT……………………………………….. 0657072588/0768516188
AGE……………..18+ 

SEHEMU YA 3 KATI YA 10

 


 

“Safi, je vikosi vya ardhi?”

“Kwenye vikosi vya ardhi mkuu tuna wanajeshi zaidi ya laki mbili, ila wajeshi elfu kumi wana mafunzo ya hali ya juu ya kikomandoo na wengine wana mafunzo ya kawaida”

“Ninahitaji zitoke ndege nne jeti na moja kubwa. Utaagiza makomandoo kumi tu, na wanajehsi wa hamsini”

“Jenero ila hiyo ni namba ndogo sana?”

“Vita ni akili na si wingi wa watu, je muna vifaa vya mawasiliano ya moja kwa moja?”

“Ndio mkuu”

“Nitahitaji kuongozana na kundi hilo la makomandoo”

“Mkuu!!”

“Nimesema andaeni vikosi, tunakwenda kupambana. Meja kamlete mke wangu”

“Sawa”

Wanajehsi hawa wakatoka chumbani hapa, nina imani kila mmoja ananishangaa kwa maamuzi yangu ya kuhitaji kuelekea kwenye mapambano haya ambayo ni hatari. Ila mimi mwenyewe ninaelewa kwamba raisi wa Marekani sasa ameamua kupambana nami.

 

“Peter kwa sasa hapana, huwezi kwenda popote mume wangu”

Yemi aliingia huku akizungumza, nyuma yake akiwa ameongozana na Meja ambaye ninaimani kwamba atakuwa amemueleza juu ya hali halisi iliyopo hivi sasa.

“Mke wangu hakuna jinsi ya kufanya ni lazima niende kupambana na vijana wangu”

“Sitaki Peter, kama ni kukuingilia katika hili basi acha nikuingilie, sinto hitaji kukupoteza na wewe, unataka mimi niishi maisha gani, unahitaji mimi niwe mkimbizi, niwe mjane si ndio”

Yemi alizungumza huku machozi yakianza kumlenga lenga, kwa ishara nikamuomba meja kutoka ofisini humu, akati amri na nikabaki na Yemi.

 

“Peter hembu angalia, hayajapita hata masaa sita tangu nimzike baba yangu, wewe nawe unataka pia nikuzike kwa nini lakini huitaji kuangalia umuhimu wako kwenye maisha yangu”

“Mke wangu hii sehemu kwa sasa sio salama, ni lazima niende nikawazuie maadui zetu huko walipo kuwa”

“Siwezi kusema kweli, ni bora kufia hapa kuliko kwenda huko unapo taka, tafadhali mume wangu, sina mtu mwengine zaidi yako wewe”

Yemi alizungumza kwa upole na machozi yakaanza kumiminika usoni mwake

“Nakupenda Peter, usiniache peke yangu, uliniahidi utaishi karibu na mimi, tunza basi ahadi yako”

Nikakaa kimya huku nikimtazama Yemi usinu mwake, taratibu nikajikuta nikimshika mkono wake wa kulia na kumsogeza karibu yangu.

 

“Nimekuelewa mke wangu sinto kwenda”

“Kweli?”

“Ndio mke wangu, ila vita ikizidi itabidi nisimame mimi kama jenero”

“Sawa mume wangu”

“Niitie meja”

Yemi akanipiga busu la mdomoni, kisha akaanza kutemba kwa haraka hadi kwenye mlango wa kuingia, akaufungua nikamkuta meja na wanajeshi wezake wakiwa wamesimama. Nikawaruhusu kuingia wote kwa ishara.

“Mkuu vikosi vipo tayari”

“Sawa”

“Wanasubiria amri yako muheshimiwa”

“Sawa wanaweza kwenda, wahikikishe wanawasiliana na wanajeshi walipo msituni wanao endesha oparesheni ya kumsaka K2”

“Sawa mkuu”

Meja akawapatia amri wajaeshi hao wanao kwenda kuhakikisha kwamba wanaangusha majeshi ya Wamarekani na jeshi la taifa hapa Nigeria.

 

“Muheshimiwa unatakiwa kuelekea katika chumba namba moja cha mawasiliano”

“Sawa”

Tukatoka chumbani hapa na moja kwa moja tukaelekea kwenye chumba hichi ambacho ndio mara yangu ya kwanza kuingia. Ukuta mkubwa wa humu ndani umefungwa Tv kubwa inayo onyesha wajaneshi hao jinsi wanavyo kwenda kupambana na kila kwenye kofia ya mwanajeshi walioenda vitani, ina kamera ndogo.

“Mumeweza kuwaona vikosi vya Wamarekani?”

“Ndio mkuu, ila bado ndege zao hatujaziona”

“Ja anga la hili eneo lina ulinzi wa kutosha?”

“Ndio jenero kuna mabomu maalumu ambayo yanaweza kuangusha ndege ya aina yoyote ambayo  inaweza kukatiza katika hili eneo”

“Basi hakikisha kwamba ndege yoyote ambayo itakuwa si ya kwetu munaiangusha”

“Sawa jenero”

Wanajeshi wetu wakazidi kusonga mbele, nikawaona wanajeshi wa kimarekani wakiwa katika vikosi vinne na wamejificha sehemu ambayo nina imani ndani ya muda walio jipangia basi wanatuvamia.

 

“Jenero tumefika sehemu ya karibu je tunaweza kushambulia”

Rubani mmoja alizungumza akiwa katika ndege yake.

“Watawanyisheni kwanza kwa risasi?”

“Mkuu!!”

“Nina maana yangu meja”

Ilibidi kumkatisha meja kwa kile anacho kishangaa.

“Fanyeni hivyo”

Marubani wakaanza kushambilia eneo walilopo wanajeshi wa Marekani na Nigeria kwa kutumia risasi za moto, jambo lililo wafanya wanajeshi hao kutawanyika huku wakishambulia ndege hizo. Uzuri wa ndege hizi zina kasi kubwa jambo ambalo ni gumu sana kwa wanajeshi wa kawaida kuweza kuzifikia katika mashambulizi.

Ndege za kijeshi za Kimarekani zikaanza kushambulia, kwani kuna sehemu zilikuwa zimejificha karibu kabisa na wanajeshi hawa walipo kuwa wamejificha.

“Tumieni mabomu sasa”   

“Sawa jenero”

“Meja umeona maana yangu. Nilihitaji kuziona hizo ndege, na kama wangetumia mabomu wale wanajeshi wasinge weza kuomba msaada, ila wametumia risasi na wanajeshi baadhi wameomba msaada kutoka kwenye hicho kikosi cha anga, kwa hiyo akili katika swala la mashambulizi ndio jambo la msingi kuliko nguvu”

 

“Nimekuelewa jenero samahani kwa hilo”

“Usijali meja”

Kwa haraka haraka unaweza kusema ni filamu moja ya kivita tunayo izungumza, ila ni uhalisia kabisa, kwani atakaye kufa kwenye mapambano hayo harudi tena duniani. Wamarekani kusema kweli wamechanganyikiwa kwani hata ndege zao za kivita zina angushwa moja baada ya nyingine kwa maana hawakujipanga vizuri na hili tulilo fanya ni shambulizi la kustukiza na nina imani litamtia presha raisi Donald Bush pamoja na Hawa ambao wamepanga kuniua na mimi sinto kubali kufa hadi nafsi zao ziweze kuonja mauti na nipo tayari hata kuanzisha vita ya tatu ya dunia, kwani Simba achezewi sharubu.



Kwa mbinu niliyo itumia haikuchukua hata lisaa, tayari tukawa tumesambaratisha mipango ya wanajeshi wa kimarekani na jeshi la serikali la hapa Nigeria.

“Jenero tumefanikiwa kuangamiza wote”

Mmoja wa marubani ambaye ndio kiongozi wa jeshi la anga alizungumza na kutufanya wote tulipo ndani ya chumba hichi kuanza kushangilia kwa furaha kwani ni ushindi ambao tumetumia akili nyingi kuliko nguvu kubwa. Taratibu Yemi akanikumbatia huku akinipiga mabusu mfululizo usoni mwangu.

“Jenero tuambie ni lini tuandae harusi yenu”

Meja alizungumza huku akiwa amejawa na tabasamu usoni.

“Mmmmmm, tutalipanga ngoja kwanza hizi sekeseke zipite”

“Sawa jenerali”

 

“Kukipambazuka nitahitaji kuzungumza na wanajeshi wote”

“Sawa jenerali”

Nikawaaga watu waliomo humu ndani ya hichi chumba, tukatoka ndani humu nikiwa nimeongozana na Yemi.

“Kusema kweli ninazidi kujisikia kwamba mimi ni mwanamke mwenye bahati sana kuwesza kupata mwanaume kama wewe, yaani nina jutia ni kwa nini nilichelewa kukufahamu mume wangu”

“Mungu atusaidie mke wangu kwa maana kwa sasa nina imani dunia mzima ni lazima itakuwa inalitafuta hili kundi na kulizungumzia”

“Usijali mume wangu, nitahakikisha ninakuunga mkono kwa kila jambo”

“Maswala ya uwanamitindo vipi?”

“Uzuri kampuni yangu inaweza kujiendesha hata kama mimi sipo karibu nao”

“Sawa mke wangu. Ila kuna kitu ambacho ninahitaji kukushauri ila sijajua kama utakubaliana nami”

“Zunngumza tu mume wangu, uzuri ni kwamba kwa sasa sisi ni kitu kimoja, japo hatujafunga ndoa ila ninaimani siku yoyote tutufunga ndoa”

 

“Kweli, ninahitaji mwanao aweze kurudi hapa Nigeria, sinto hitaji akae mbali nasi, nahitaji aanze kunizoea mimi kama baba yake mpya”

“Niwazo zuri ila hapa Nigeria ninajua atawindwa na wabaya, kwa maana ninaimani kwamba lazima serikali inafahamu kwamba baba yangu ndio muhusika mkubwa wa hili kundi”

“Nitahakikisha tunamlinda kwa hali yoyote, kwa maana kukaa kwake mbali kunanifanya nikose amani kabisa”

“Usijali mume wangu”

“Martin asante kwa kutuleta hapa nenda kapumzike”

“Sawa mkuu”

Martin akatuacha nje ya mlango wa chumba chetu, tukaingia ndani huku sote tukiwa tumechoka sana.

“Haki ya Mungu, leo imekuwa siku ndefu sana jamani”

Yemi alizungumza huku akijirusha kitandani na kulala chali. Taratibu nikaanza kuvua nguo zangu, huku nikijitazama kwenye kioo cha kabati hili.

 

“Hivi Peter hili jeshi mulilo liangamiza leo hawato rudi tena kutuvamia?”

“Kurui kutuvamia lazima watarudi tu”

Taratibu Yemia akanyanyuka na kukaa kitako huku sura yake ikonekana kujawa na wasiwasi mwingi sana.

“Usijalili mke wangu nina imani tutashinda, mtu akitufwata tunahaki ya kumpiga kwa maana tukimuacha atatupiga sisi”

“Sawa mume wangu”

“Itabidi kuomba msaada kwenye nchi ambazo zina uadui na Marekani”

“Nchi kama zipi?”

“Ya kwanza ni Urusi, hawa ninajua hawapatani kabisa na Marekani, nchi ya pili ni Korea ya Kaskazini, nitahijitahidi kukutana na wakuu wao wa nchi na nitawaleza lengo letu”

“Pia kuna nchi kama Pakistani, Iraqu pia hao unaweza kuwaomba msaada mume wangu”

 

“Yaaa najua Marekani akirudi kwa mara ya pili hato kuja kwa kujitega tega kama alivyo fanya, akija atakuja kwa kushambulia tena kwa mabomu makubwa makubwa. Anaweza hata kutumia nyuklia japo anapiga vita zisitumike duniani”

“Mungu wangu sasa kama akiamua kutumia nyukilia si tutupotea katika ulimwengu huu pasipo kutimiza malengo ya baba?”

“Usijali mke wangu, ninajua cha kufanya hilo wala wewe lisikusumbue”

“Sawa mume wangu”

Nikamshogela Yemi kitandani alipo lala. Taratibua nikaanza kumvua nguo zake huku nikimtazama usoni mwake kwa macho yaliyo jaa mahaba.

“Ujachoka mume wangu tuu…..?”

“Kwenye hili siwezi kuchoka”

“Mmmmmm jamani kwa hiyo huku hata ukiwa hoi nyang’anyang’aaa wewe huto choka kabisa kupana……”

Nikawahi kumzima mdomo Yemi kwa kutumia lipsi zangu, taratibu tukaanza kuchezesha ndimi zetu.

Tukaanza kupeana burudani , hatukutumia muda mwingi tukamaliza burudani yetu. Tukashuka kitandani na kuingia bafuni, tukaoga na kurudi chumbani hambapo hatukuwa na mazungumzo mengi sana, tukajikuta tukilala fofo.

                                                                                                    ***   

Mlio wa simu ya Yemi ukanistua kutoka usingizini, taratibu nikafumbua macho yangu na kuichukua, sikutaka kuipokea kama utaratibu tulio jiwekea, hakuna mtu ambaye anaishika simu ya mwenzake.

“Yemi, Yemi”

“Mmmmm”

“Simu yako inaita”

“Nani tena asubuhi yote hii?”

Yemi aliuliza huku akijinyanyua kidogo kitandani akaichukua simu na kuitazama kwa muda kisha akaipokea. Taratibu nikashusha kitandani, nikapiga hatua hadi kwenye dirisha, nikafungua pazia na kutazama nje. Wanajeshi wangu wanazidi kufanya mazeozi ya viongo.

“Wewe ni nani?”   

Sauti ya ukali ya Yemi ikanifanya nigeuke nyuma na kumtazama.

“Mwanangu yeye wa nini?”

Yemia lizidi kuzungumza kwa ukali na kunifanya nianze kutembea taratibu kurudi kitandani huku nikiwa sina hata nguo moja kwenye mwili wangu. Nikaanza kumuona Yemi machozi yakianza kumwagika usoni mwake.

“Mke wangu kuna nini kimetokea?”

Yemi hakunijibu zaidi ya kuendelea kulia, kwa haraka nikampokonya simu yake na kuiweka sikioni mwangu.

“Mamaa……”       

Niliisikia sauti ya mtoto mdogo wa kiume, akiita moja kwa moja nikagundua kwamba atakuwa ni mtoto wa Yemi.

“Tunahitaji Dany ajisalimishe na tumuachie mwanao”

Niliisikia sauti ya kiume ikizungumza.

“Wewe ni nani?”   

Nilizungumza kwa sauti nzito huku nikiwa nimekasirika sana.

“Ohooo Dany nashukuru kupokea simu yako”

“Nimekuuliza wewe ni nani?”

“Mimi ni rafiki yako wa muda mrefu sana. Hongera kwa kuoa”

“Nimekuuliza wewe ni nani ambaye unajaribu kuingia kwenye maisha yangu”

 

“Mimi ni Donald. Donald Bush”

Mapigo ya moyo yakaanza kunienda mbio sana baada ya kusikia sauti halisi ya raisi wa Marekani, kwani hapo mwanzo sauti yake ilikuwa nzito naamini alijaribu kuibadilisha ili isiweze kujulikana kirahisi.

“Unahitaji nini?

“Ninakuhitaji wewe Dany, yaani leo hii wewe ndio mkuu wa Al-Shabab wakati nilikutuma ukafanye kazi ya kuangamiza kundi hilo”

Nikatamani kufoka ila nikabaki nikiwa nimemtazama Yemi na kushindwa kuzungumza chochote kibaya kwa raisi huyu ambaye kusema kweli kwa sasa amevuka mpaka ambao sidhani kama ataweza kurudi upande wa pili alipo toka.

“Lini na wapi unahitaji nijisalimishe”

“Hahaaaa, umekuwa mnyonge sana kwa ajili ya mtoto wa mwanaume mwenzako. Tafuta wa kwako basi, usililile watoto wa wezako”

 

Nikazidi kujizuia kutokuzungumza neno baya ambalo Yemi anaweza kulisikia hapa.

“Huyo ni mwanangu, niambie ni wapi na saa ngapi utahitaji nijisalimishe mikononi mwako na umuachie mwanangu?”

“Lazima uje Marekani, na ninakupa masaa arobaini na nane, yaani siku mbili uwe umesha fika ndani ya Marekani na ukifika hapa nitakuambia ni wapi na saa ngapi utaweza kumpata mtoto ambaye si wako”

“Nimekuelewa”

Nikakata simu huku machozi ya hasira yakinilenga lenga usoni mwangu huku kifua changu kikianza kuvimba kwa hasira hii.

“Mwanangu wamemteka”

Yemi alizungumza huku akiendelea kulia kwa uchungu. Nikaichukua suruali yangu iliyopo juu ya sofa, nikavaa kwa haraka, nikachukua tisheti ndani ya kabati na kuvaa. Nikaanza kutembea kuelekea mlangoni huku nikiwa nimeishika simu ya Yemi mkononi mwangu.

“Dany”

Yemi alinita kwa jina ambalo sikuwahi kumuambia hata siku moja. Nikajikuta nikiwa nimesimama mlangoni huku nimeshika kitasa cha mlango.

 

“Dany ndio jina lako halisi Peter?”

Nikayafumba macho yangu huku nikijaribu kupambana katika kuipunguza hasira yangu kwani ninashindwa hata kuzungumza kabisa.

“Naomba unijibuuu”

Yemi alizungumza kwa hasira na kunifanya nigeuke na kumtama kwa macho makali. Nikaanza kutembawa kwa kujiamini huku nikimfwata kitandani alipo kaa. Yemi taratibu akaanza kuudi nyuma huku akiwa na wasiwasi mwingi usoni mwake.

“Ndio ni jina langu”

Nilizungumza kwa sauti nzito huku nikijaribu kuibana pumzi yangu inayo kifanya kifua changu kupanda na kushuka kwa ajili ya hasira.

“Kwa nini ulinidanganya eheeeee?”

Yemi alizungumza huku akiendelea kulia kilio  kikali.

“Tazama sasa  mwanangu wamemteka, tazama Peter kwa nini hukuniweka wazi kwa nini hukuniweka wazi eheeeee”

Yemi alizungumza huku akianza kunipiga vibau vya mashavuni mwangu. Sikutaka kumfanya chochote zaidi ya kuendelea kumtazama na kumucha azidi kunipiga makofi yake.

 

“Wananitaka mimi na si mwano, nitahakikisha mwanao  anarudi mikononi mwako”

“Kivipi Peter, wewe ni muongo umenidanganya mimi, umemdanganya baba, umewadanganya wanajeshi w…….”

“Yemi kimya”

Nilizungumza kwa kufoka na kumfanya Yemi kutetemeka mwili mzima huku akiwa amenitola macho yake kwani nina imani hakuwahi kunifumania nikiwa katika hasira kama hii niliyo nayo hivi sasa.

“Wewe na baba yako majina munayo yatumi ni halisi, eheeeee? Muliwa kuniambia majina yenu halisi eheeee?”

Nilimfokea Yemi na kumfanya akae kimya huku machozi yakimtiririka mashavuni mwake hata sauti ya kilio nayo ikakatika.

 

“Sisi sote katika hili ni waongo, baba yako amekufa na siri yake na wewe umekaa na siri hiyo hata siku moja hhukuwahi kuniambia siri yenu ambayo nimeifahamu hata kabla ya kuja hapa Nigeria”

“Na nimekuwa msaliti kwa wale walio kuwa wamenituma kwa ajili yako wewe, na laiti ningeihitaji kuwaua wewe na baba yako pasinge kuwa na mtu wa kunizuia kufanya hivyo. Ila wao walisaliti na ndio maana nikawa na nyinyi, ndio maana ninahitaji kuhakikisha ninalipa kisasi kabla sijaingia ndani ya hii ardhi. Nitaleta mwanao mikononi mwako, na kuanzia hapo nitakuwa tayari kufa na kuifwata familia yangu kule ilipo elekea ambayo K2 amehusika katika kuwaua”

Nilizungumza kwa hasira na sauti ya ukali huku nikiwa nimemtazama Yemi usoni mwake, na jambo lililo pelekea kuzungumza maneno ambayo sikuyatarajia kuyazungumza mbele ya Yemi siku hata mmoja kwenye maisha yangu.



“Kifo changu hakito kuwa na thamani kwa mtu yoyote, maisha yangu yalisha haribika tangu nikiwa kijana mzuri ambate laiti kama ningekuwa nimetulia leo hii nisinge kuwa hapa na kuingia katika mikasa kama hii ambayo unaiona. Nimeteseka, nimegangaika, bado napigana kuhakikisha kwamba ninalipa kisasi kwa wale ambao  wameiteketeza familia yangu”

Nilizungumza huku machozi yakinitoka usoni mwangu.

“Najua nitakufa, Marekani inaniwinda mimi, Tanzania inaniwinda mimi, nilazima nitakufa mke wangu, mimi sio mwanaume wa kunipenda kwa maana sina gerentii ya maisha yangu”       

“Hapana Peter usizungumze hivyo, ninakupenda”

“Ninanjua unanipenda ila maisha yangu ni ya hatari, sina makazi maalumu Yemi, siwezi kusema ninaweza kuanzisha familia ambayo inaweza kuingia matatizoni kisa mimi. Hembu tazama familia yangu iliuwawa kwa kuchinjwa, tazama mwanao kwa sasa ametekwa kwa ajili yangu, bado unihisi kwamba mimi ni mwanaume sahihi kwenye maisha yako?”

Kwa haraka Yemi akanisogelea na kunikumbatia kwa nguvu huku akimwagikwa na machozi usoni mwake.

“Peter wewe ndio mwanaume wa ndoto zangu, nina kuahidi tutakuwa pamoja kufa na kupona, ninakupenda sana, ninakuhitaji kwenye maisha yangu wewe ndio baba wa wanangu. Lolote litakalo tokea nipo pamoja na wewe, kamwe sinto jali ni nani anaye kuwinda anaye kutafuta ila nitahakikisha kwamba ninakuwa na wewe mume wangu”

Maeno ya Yemi yakazidi kunisisimua mwili wangu, taratibu tukaachiana huku tukitazamana.

“Ninatakiwa kulishuhulikia swala la mtoto, ninakuomba utulie na nitajua nitakacho fanya”

“Kwani mume wangu hao walio mshikilia ni kina nani?”

“Aliye mshikilia ni mtu mmoja na ananguvu kubwa sana kwenye huu ulimwengu”

“Ni nani huyu mume wangu?”

“Ni raisi Donald Bush, ni raisi wa Marekani?”

Yemi akaonekana kustuka kidogo, mstuko wake ninatambua unatokkana na mtu niliye mtajia.

“Kwenye hiyo vita ni lazima na mimi nipigane kufa na kupona”

Yemi alizungumza kwa msisitizo huku akinitazama usoni mwangu.

“Kwa nini?”

“Nilijua kwamba huyo mshenzi atakuwa ameacha kuiandama famili yangu kumbe bado anendelea kuiandama ni lazima nimuue”

Yemi alizungumza kwa msisitizo na kuzidi kunishangaza.

“Ni kitu gani ambacho unakifahamu dhini ya Donald Bush?”   

Yemi akaka kimya kwa muda huku akionekana kufikiria jambo fulani kichwani mwake.

“Niambie mke wangu?”   

“Donald Bush alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na mama yangu, kabla mama hajakutana na baba yangu, baada ya wawili hao kuachana chuo kila mmoja kuendelea na maisha yake, mama aliweza kumpata baba. Basi Donald alijaribu sana kumrudisha mama mikononi mwake, ila mama alisha mpenda baba yangu, mwisho wa siku katika kugombania msichana na kupambana na baba, alimchoma mama kisu cha tumbo kisha akamchoma na baba kisu cha tumbo, sikuweza kufanya chochote nilipo shuhudia tukio hilo kutokana mimi nilikuwa bado mdogo mdogo. Mama alifariki ila baba aliweza kubaki hai. Baada ya kupona ndipo baba alipo anza harakati za kutengeneza jeshi lake hadi leo unaona jeshi limekuwa kubwa kama hivi”

“Baba alijaribu kulipiza kisasi?”

“Waliwindana sana, hadi baba amefariki hakuweza kufanikiwa kumpata, na wala mimi sikujishuhulisha na maswala ya kulipiza kisasi kwani niliamua kuishi maisha ya usalama na ya amani. Ila kwa hapa alipo fika, amefikia pabaya sana, ni lazima nimshuhulikie”

“Yemi”

“Bee”

“Una nipenda?”

“Ndio ninakuependa mume wangu, zaidi ya unavyo fikiria”

“Una niamini?”

“Ndio mume wangu”

“Ninakuomba hili swala nilishuhulike mimi peke yangu, sihitaji wakuguse wewe”

“Dan……ahaa Peter”

“Ukipenda kuniita Dany pi unaweza kuniita mke wangu hakuna haja tena ya kuficha uhalisia wangu kwako ikiwa unafahamu kila kitu”

“Sawa mume wangu. Ila kumbuka kwamba mimi na wewe ni mke na mume na tunatakiwa kushirikiana ili kumkomboa mtoto wetu?”

“Natambua hilo ila ninakuahidi mtoto atarudi, na nitakuacha hapa na utaweza kusimamia madaraka yote ya kijeshi na amri ya mwisho watapokea kutoka kwako sawa mke wangu”

“Dany mimi na jeshi wapi na wapi?”

“Najua unaweza, na ninatambua utafanya. Huu sio wakati wa kurudi nyuma mke wangu, huu ni wakati wa kupambana sawa”

“Sawa mume wangu”

“Ngoja nielekee nje sasa”

Nikambusu Yemi usoni mwake kisha nikashuka kitandani, nikaanza kueleka nje huku nikiwa nimeishia simu ya Yemi mkononi mwangu.

“Habari ya asubuhi jenero”   

Martin alinisalimia mara baada ya kutoka chumbani kwangu na kumkuta akiwa amesimama sebleni akinisubiria.

“Salama tu, kuna lipi jpya?”

“Hakuna jipya ila wanajeshi wanaisubiria hotuba yako kwa hamu sana”

“Usijali majira ya saa nne nitawahutubia, ila kwa sasa muambie meja aje ofisini kwangu nina mazungumzo naye”

“Sawa mkuu”

Tulizungumza huku tukitembea, Martin akaeleke kumuita meja na mimi nikaelekea ofisini kwangu. Nikaingia ofisini kwangu, na kukaa kwenye kiti changu huku mawazo mengi yakiendelea kunitawala kichwani mwangu. Hisia zangu za kukataa mtoto wa Yemi kuishia mbali nasi kumbe zilikuwa sahihi kabisa. Mlango ukafunguliwa akaingia meja, akanipigia saluti kwa ishara nikamruhusu kukaa kwenye kiti kinacho tazamana nami.

“Jenero mbona unaonekana huna furaha kabisa?”

“Kuna tatizo ila hili ni binafsi sana, sitaki kulihusisha jeshi kwani sihitaji mtu yoyote aumie tena kwa ajili yangu”

“Tatizo gani jenero”

“Mtoto wangu wa kufika amekamatwa na Wamarekani”

“Mtoto wako wa kufikia!!?”

Meja aliniuliza huku akiwa amenitazama usoni mwangu.

“Ndio, mtoto wa Yemi amekamatwa na raisi wa Marekanani na ananishinikiza mimi kwenda kufanya mabadililo naye la sivyo atamuu”

“Mke wako anatambua hilo?”

“Yeye ndio alikuwa wa kwanza kuweza kulitambua hilo swala”

“Duuuu”

Meja alizungumza huku akishusha pumzi nyingi kwani hili swala ni zito sana na linahatarisha maisha yangu na usalama wa hili jeshi kwa asilimia tisini, kwani nimesha anza kuona jinsi mchango wangu ulivyo mkubwa kwneye hii chini.

“Yaani hapa kichwa changu kina niuma, mke wangu ana kazi ya kulia tuuuu, yaani ninashindwa kabisa nifanyaje, na nimekwama kusema kweli meja wangu”

“Unaonaje hiyo kazi tukawapa vijana wetu wakaifanya?”

“Hapana Mmarekani akiwa kwake ana mbinu nyingi sana za kuwakamata, na hiyo inaweza kupeleka vijana wetu wakapoteza maisha kwa swala ambalo haliwahusu”

“Ila jenero kumbuka kwamba hapa huyu ni mjukuu wa muasisi wa hili kundi, ni lazima damu yake ipiganiwe kwa garama yoyote”

“Hilo ni kweli ila sinto hitaji iwe hivyo”

“Sasa hapo tunafanya nini jenero wangu?”

Sijui meja, yaani natamani kwenda kuifanya hii kazi ila sinto rudi, hawa watu zaidi ya laki mbili wataongozwa na nani?”

Sote tukajikuta tukikaa kimya huku tukikuna vichwa vyatu.

“Nimekumbuka kuna watu wanaweza utuusaidia”

Maje alizungumza na kunifanya nimtazame usoni mwake.

“Kitu gani?”

“Kuna kundi moja la majasusi lipo Mosscow nchini Urusi, hilo lina mtandao mkubwa sana hadi ndani ya serikali ya Marekani, kwa kuwatumia hao mtoto anaweza kurudishwa akiwa salama Salmin na kikubwa ambcho kinatakiwa ni kuweka pesa mezani”

“Unaweza kuwasiliana nao hata sasa hivi?”

“Ndio ninaweza mkuu”

“Wasiliano nao basi tujue tunafanyaje”

Meja akatoa simu yake mfukoni akaminya minya batani za simu yake na kuiweka sikioni. Meja akaanza kuzungumza na mtu huyo.

“Ndio tulipata msiba wa mzee jana ndio tumemzika”

“Tunashukuru, ila kuna tatizo moja kubwa sana”

“Mjukuu wa mzee ameshikiliwa na serikali ya Marekani, wanamshinikiza mkuu wetu mpya aweze kujisalimisha mikononi mwao na watamuua nina imani wakimkamata”

Kwa ishara ninakumuomba meja kuweka simu yake loudspeaker.

“Mumepata mkuu mpya?”

“Ndio tnaye mkuu mpya ni mkwe wa mzee”

“Yule jamaa bishoo bishoo”

“Hapana huyu wa sasa ni komandoo, naamini umesikia jinsi tulivyo mtandika mmarekani na jeshi la Nigeria, yote nimatunda yake”

“Kama ni yeye aliye ongoza basi mumepata kichwa hapo”

“Yaaa, sasa anahiyaji hii uparesheni muifanye nyinyi, je mutaweza?”

“Hakuna jambo linalo shindikana hata kama mukihitaji tumuangamize huyo aliye mshikilia tunaweza kufanya”

“Basi zungumza naye huyu hapa”

“Habari yako ndugu”

Ilinibidi nianze kuzungumza mimi.

“Salama jenero hongera kwa ushindi wako wa jana, dunia nzima inalia kwa kile mulicho kifanya ila kwetu sisi ni furaha kwa maana tumepata wasaidizi wetu kwenye hii na Mmarekani”

“Ninashukuru sana, kitu ninacho kihitaji munifanyie ni kuhakikisha mwanangu anarudi mikononi mwangu nyinyi niambieni ni kiasi gani cha pesa mutahitaji ili kumkomboa mtoto wangu”

“Kwa sasa kaka sihitaji pesa yako, ngoja tuifanye kazi ikikamilika basi nitakuambia ni kiasi gani ambacho tunahitaji na pia nitahitaji ushirikiano wetu, kwani vita yetu sote ni dhidi ya Marekani”

Maneno ya huyu kiongozi wa kikundi cha kijasusi yakanifariji snaa moyoni mwangu na kujikuta nikishusha pumzi huku  nikitokea kuwaamini sana katika utendaji wao wa kazi japo sikuwahi kuwaona nah ii ndio mara yangu ya kwanza kuwasikia.



“Nimekuelewa ndugu na mutachukua muda gani kuweza kukamilisha zoezi la kumuokoa mwanangu?”

“Masaa kumi na mbili kuanzia hivi sasa, tupatie picha ya mwanao kisha tunajua tunaanzia wapi?”

“Poa poo tutakutumia baada ya muda mfupi”

“Sawa mkuu”

Nikakata simu na kumrudishia meja simu yake huku usoni mwangu nikiwa nimejawa na tabasamu pana kiasi kwani nimepata njia ya matumaini.

“Naomba ukaniitie mke wangu”   

“Sawa jenero”

Meja akatoka ofisini kwangu na kuniacha nikiwa ninatafakari njia ya pili enepo majasusi hawa watashindwa kabisa kumukoa mtoto wa Yemi. Haukupita muda sana mlango ukafunguliwa akaingia meja pamoja na Yemi ambeye usoni mwake amapoteza furaha kabisa. Taratibu Yemi akaka kwenye kiti alichokuwa amekali na meja na kumfanya meja kusimama.

“Mke wangu tuepata njia ya kumuokoa mtoto”   

“Njia gani mume wangu?”   

Nikatamzama meja na kumpa ishara ya kuelezea mpango mzima tulio upanga na majasusi wa Urusi.

“Muna waamini?”   

“Ndio nina waamini wamefanya kazi nyingi pia na marehemu baba yako, na kupitia baba yako mimi niliweza kuwafahamu”

Meja alizungumza kwa kujiamini  sana.

“Sasa wanataka kiasi gani?”

“Hawaitahi kiasi chochote kwa sasa hadi kazi itakapo kamilika, ila wamehitaji picha ya mtoto wetu”

“Tuwapatie kama ndio hivyo?”

Yemi alizungumza kwa sauti iliyo jaa upole ndani yake huku akinitazama usoni mwangu.

“Sawa meja unaweza kufanya hilo”

“Naomba simu, kuna picha niliyo tumiwa whatsapp wiki iliyo pita nia imani itakuw andio nzuri”

Nikamkabidhi simu Yemia akaanza kuitafuta picha hiyo kisha akanigeuzia simu niitazame picha hiyo.

“Inafaa. Meja chukua simu hiyo umtumie jamaa”

“Sawa jenero”

Meja akachukua simu ya Yemi, akatoka humu ofisini. Taratibu nikasimama na kumsogelea Yemi ambaye hana furaha kabisa kwenye uso wake. Taratibu nikamnyanyua huku nikimkumbatia tararibu pasipo kuzungumza kitu chochote.

“Dany mume wangu ninakupenda sana”

“Ninakupenda pia mke wangu”

“Nikuulize kitu?”

“Niulize”

“Kama ingekuwa hujasalitiawa na watu walio kuwa wamekuagiza ni kweli ungetuua?”

Swali la Yemi likanifanya nikae kimya kwa sekunde kadhaa huku nikifikiria kile nilicho kifanya kwa baba Hawa na kundi lake la Al-Shabab.

“Nisinge weza kufanya hivyo?”

“Kwa nini?”

Yemi alizungumza huku akijitoa mikononi mwangu taratibu na kunitazama usoni mwangu kwa macho ya mshangao kidogo.

“Ninakupenda, na mulinipenda na kuniamini, hata kama wasinge kuwa wamenisaliti kama ulivyo sema ila ukarimu wenu ungeyayusha maagizo yote niliyo kuwa nimepewa dhidi yenu”

“Nashukuru sana mume wangu kwa hilo kwa mana umesha tambua ukweli ni kwamba ulikuwa unatumiwa kulipiza kisasi cha watu wengine ikiwa wao wamekaa kwenye sehemu zao salama salimini”

“Usijali mke wangu, ndio manaa ninahitaji jeshi la baba yako kwa sasa lifanye kazi za faida, na zilizo njema na si kwa kuwaumiza wananchi wasio na uwezo wa kijeshi”

“Ni kweli unatakiwa kufanya mabadiliko mume wangu wewe ni kijana na wengi walipo kwenye hili kundi ni vijana wezako wape maisha ambayo kila mmoja atakupenda na kukuheshimu zaidi ya hapa wanavyo kuheshimu”

“Asante mke wangu kwa ushauri wako”

Mlango ukagongwa kwa nje taratibu nikamuachia Yemi na kumkaribisha mtu anaye bisha hodi. Akaingia Martin akiwa ameshika faili.

“Muheshimiwa nimekuandalia hotoba kama hotojali unaweza kuipitia”

Martin alizungumza huku akikabidhi faili hili alilo kuja nalo ofisini kwangu.

“Shukrani”

Nilizungumza huku  nikilichukua faili hili na kulifunua, nikaanza kupitia mwanzo wa hii hotuba, nikamtazama Martin kisha nikatabsamau kwani kile alicho kiandika ni kama vile alikuwa kwenye akili yangu kwani niliahidi kuhutubia wanajeshi wangu kwa ushindi tulio upata ila kwa haya matatizo niliyo kutana nayo asubuhi ya leo kichwa changu chote kimepagawa na sijui ni kitu gani ninaweza kukifanya.

“Umefanya jambo zuri Marti, waambie wanajeshi baada ya nusu saa nitakuwa uwanjani kwa ajili ya kuwahutubia”

“Sawa”

Akaingia meja, Martin akatoka na kutuacha ofisini.

“Nimesha mtumia mkuu”

“Amesemaje?”

“Ameomba nimpigie azungumze na wewe”

“Mpigie”

Nilizungumza huku nikizunguka meza hii na kukaa kwenye kiti changu, meja akapiga simu kwa mkuu wa kikosi cha majasusi kisha akanikabidhi.

“Ndio kaka”

“Tumeipata picha ya mwanao, na upelelezi tulio ufanya hadi hivi sasa, mwanao ameshikiliwa katika ikulu ya Marekani na sehemu hiyo inahitaji nguvu ya ziada kuweza kuingia hapo ikulu”

“Ohoo Mungu wangu”

Nilizungumza huku nikishusha pumzi nyingi, jambo lililo mfanya Yemi kunitazama kwa macho ya mshangao huku  akiwa na shauku ya kuhitaji kuni kitu gani kinacho endelea.

“Ni pagumu sana kuweza kuingia ndani ya ikulu ya Marekani, kwani sasa hivi ulinzi wake umebadilika kwa asilima mia moja, na kufanya hivyo inaweza kuepela vijana wangu wengi kupoteza maisha”

“Hamna mtu ndani ya ikulu ambaye anaweza kuifanya hiyo kazi?”

“Yupo ila nimewasiliana naye inavyo onyesha ni kwamba hato weza kufanya hivyo kwani mtoto wenu yupo chini ya ulinzi wa askari wa raisi na nikatika chumba cha siri”

“Naomba unipe dakika kumi na tano nitakupigia”

“Sawa kaka”

Nikakata simu huku nikiwa nimepiteza furaha kabisa kwenye uso wangu.

“Mume wangu naomba uniambie ni kitu gani ambacho kimempata mwanangu?”

“Yupo ndani ya ikulu ya Marekani na yupo katika chumba cha siri”

“Ohoo Mungu wangu, sa…sasa wamesemaje hao watu?”

Nikamtazama Yemi usoni mwake kwa sekunde kadhaa huku nikitafakari ni kitu gani ninacho weza kukifanya.

“Mkuu hili jambo linahitaji tuandae kikosi cha kwenda kuifanya hivyo kazi?”

“Sio kwenye ikulu ya Marekani, hakuna hata mmoja ambaye anaweza kutoka salama”

“Acha tu iwe hivyo mkuu?”

“Meja kufanya hivyo pia mwanangu ninamuweka katika hali ya hatari, unahisi wamarekani wataacha kumua endapo sisi tukienda kuwavamia?”

Maneno yangu yakamfanya meja kukaa kimya kwa sekunde kadhaa huku akinitazma usoni mwangu, Yemi hakusema kitu chochote zaidi ya kuinama chini huku kiganja cha mkono wake wa kulia kikiwa na kazi ya kuziba uso wake moja kw amoja nikatambua kwamba analia.

“Ila tuna makomandoo ambao tukiwatuma nina uhakika wanaweza kuifanya hii kazi ikaenda sawa sawa”

“Meja naomba unipe muda wa kulifikiria hili na mke wangu”

“Sawa mkuu”

Meja akatoka ofisi humu na kutuacha na Yemi. Nikaanza kusikia kilio cha Yemi kwa sauti ya chini, kadri muda ulivyo zidi kwenda ndivo jinsi alivyo zidisha kulia kwa sauti.

“Mke wangu”

Nilizungumza kwa sauti iliyo jaa majonzi huku nikinyanyuka kwenye kiti changu, nikamnyanyua Yemi kweye kiti alicho kali na kumkumbatia kwa mara nyingine.

“Mke wangu nitahakikisha  kwamba ninamleta mwanao nyumbani sawa”

“Kivipi Dany hembu tazama, tazama mwanangu sasa hivi yupo ikulu ya hao mashetani, hivi kweli mwanangu atarudi jamani?”

Yemi aliendelea kuzungumza huku akilia kwa uchungu.

“Atarudi mke wangu mimi ndio ninaye kuahidi, nitahakikisha kwamba anarudi”

Niliendelea kumfariji Yemi hadi akapungumza kulia kwa uchungu, alipo maliza nikamuomba akae kwenye kiti, nikachukua faili mezani alilo niletea Martin, nikambusu Yemi kwenye paji la uso wake kisha nikatoka ofisini humu. Tukaanza kuongozan ana Martin hadi kwenye kiwanja kikubwa, nikawakuta wanajeshi wengi wakiwa wamesimama kwenye mistari iliyo nyooka vizuri.

“Muheshumiwa kila kitu kipo salama”

Meja alizungumza huku akinitazama usoni mwangu, nikawatazama wanajeshi hawa wanao nisubiria mimi kwa muda sasa, nisha taratibu nikasogelea sehemu yenye kipaza sauti huku Martin akisimama nyuma yangu. Nikaka kwa takribani dakika tano huku ninawatazama wanajeshi hawa, kichwa changu kusema kweli hakipo sawa. Usoni mwangu inanijia picha ya mtoto wa Yemi, kilio cha Yemi ninakisikia masikioni mwangu.

“Mkuu mbona kimya”

Martin alininong’onezaa kwa sauti ya chini.

“Ehee!!”

“Ipo kimya mkuu watu wanasubiria uzungumze kwa sasa”

“Sawa sawa”

Nikasha pumzi nyingi hadi ikasikika kwenye kipaza sauti kilicho wekwa mbele yangu. Nikanyoosha mkono wangu wa kulia juu huku nikiwa nimekunja ngumi.

“Bokoooo Haramuuuuu”

Wanajeshi wote wakaitikia kwa shangwem jambo lililo nipa ujasiri kidogo wa kuzungumza.

“Jana ilikuwa ni siku ndefu kwetu sote, nina imani wengi wenu mumeamka mukiwa na uchovu na kuchoka kwa namna moja ama nyingine. Tuliweza kumsindikiza mzee wetu katika nyumba yake ya milele, na pia tuliweza kuwapiga Wamarekani pamoja na jeshi la serikali la hapa Nigeria”

“Huu ni mwanzo mzuri katika uongozi wangu, mwanzo ambao nitahiji uende hivi hivi hadi pale mauiti yatakapo nichukia. Sipendi kuona damu ya hata mmoja wenu ina mwagika, yale mauaji yaliyo fanywa na raisi wa Tanzania, K2 siwezi kuyaacha yapite hivi hivi. Ni lazima na mimi nilipe kwa ubaya wake alio ufanya.”

“Jana tuliwaweza kuwazuia wavamizi wetu, ial tukumbuke ni lazima wavamizi wetu watajipanga na kurudi dhidi yetu. Ninacho waomba mukifanye, tuhakikishe kwamba tunajiandaa kwa lolote ambalo litajitokeza mbele yetu, nilazima tuhakishe tunakuwa ni kundi bora kama ilivyo kwa Al-quida”

Nikaka kimya huku nikifikiria niwaeleze juu ya kutekwa kwa mtoto wa Yemi ila nikajukuta nikijikataza mimi mwenyewe kuzungumzia jambo hilo.

“Ninaandaa mpango mzuri na viongozi wa juu, nitahakisha kwamba kila mwanajeshi anakuwa na gerentii ya maisha yeke na familia yake. Kila mwanajeshi nitahakikisha kwamba familia yake inapatiwa huduma nzuri kuanzia afya, malezi, na chakula.”

Wanajeshi wote wakashangilia na kunifanya nitabasamu.

“Mimi ni kijana mwenzenu ninaweza kuifanya kazi yoyote ambayo nyinyi munaweza kuifanya nitawaomba kama kuna wasaliti katikati ya hili jeshi basi waondoke mapema iwezekanavyo kwani sinto muonea huruma mtu ambaye ni msaliti, nitahakikisha kwamba anakufa mbele ya watu wengine kwa kupigwa risasi zisizo na idadi. Ninawatakia asubihi njema”

Baada ya kumaliza kuzungumza maneno hayo nikashuka kwenye jukwaa hil na kuwaacha wanajeshi wakinipigia makofi.

“Mkuu nimepata simu kutoka Urusi”

“Jamaa wanasemaje?”

“Wanaomba wazungumze nawe”

“Wapigie”

Nilizungumza na meja huku tukiendelea kutembea kurudi ofisi kwangu. Meja akapiga simu baada ya muda akanipatia simu yake na kunikabidhi.

“Ndio ndugu”

“Tumepata tatizo”

“Tatizo gani?”

“Mtu ambaye tulikuwa tunawasiliana naye kuweza kutupa maelekezo ndani ya ikulu ya Marekani amekamatwa na hivi sasa anahojiwa ili kuweza kutoa ushirikiano wa sisi kukamatwa”

“Nyinyi kwani mupo wapi?”

“Watu wangu wapo Marekani ila wanajiandaa kuondoka nchini hamo. Kwa hiyo ninahitaji kukuambia kwamba kazi uliyo tupa hatutoweza kuifanya kabisa. Samahani kwa hilo ndugu”

Nikabaki kimywa kwa sekunde kadhaa, huku nikiwa nimesimama, nikakata simu na kukabidhi meja simu yake.

“Hii kazi nitaifanya mimi mwenyewe, ninakuomba uniandalie usafiri ambao utanifikisha nchini Marekani kisiri pasipo mke wangu kujua wala serikali ya Marekani kufahamu.”

“Jene……”

“Meja fanya hivyo, hiyo ni amri na si ombi”

Nilizungumza kwa sauti nzito huku nikimtazama meja usoni mwake na kumfanya atingishe kichwa kukubaliana kwa kile nilicho kizungumza kwani hata akikataa hawezi kupinga maamuzi yangu kwani mimi ndio mkubwa wake wa kazi japo kiumri yeye ndio mkubwa.  



Taratibu nikaanza kuondoka kuelekea ofisini kwangu huku kichwani mwangu mawazo mengi sana. Dalili ya maisha yangu kufikia ukingoni ninaianza kuiona mbele yangu. Kwa sasa kusema kweli sinto hitaji mwanamke yoyote kunipenda na kulia kwa ajili yangu kwani ninatambua mwisho wa mapenzi yetu ni kuingia matatizoni na anaweza kupoteza maisha kama ilivyo kuwa kwa mwanamke ninaye mpenda Cajol.

“Mkuu”

Sauti ya Martin ilinistua, taratibu nikageuka nyuma na kumtazama usoni mwake.

“Kama huto jali ninakuomba nifahamu ni kutu gani kinacho endelea kwa sasa”

Nikamtazama Martin usoni mwake, kiumri nahisi nitakuwa nimempita miaka michache sana. Nikatabasamu huku mkono mmoja nikimshika begani mwake.

“Martin kuwa kiongozi lazima ni mambo mengi yanatokea, kwa hiyo usijali mdogo wangu”

 

“Ila mkuu ulisema kwamba utaniamini, tafadhali ninakuomba uniambie kwa maana naona kuna siri kubwa inayo endelea kati yako na meja na huitaji ni hata mke wako ajue. Mkuu kumbuka nilikuambia kwamba nipo tayari kufa kwa ajili yako na nipo tayari kubeba siri zako na matazo yako vyovyote itakavyo kuwa nitahakikisha ninafanya hivyo. Tafadhali mkuu naomba uniambie”

Maneno ya Martin yakanifanya mwili wangu wote kunisisimka na kujikuta machozi yakinilenga lenga usoni mwangu. Nikatamani kuzungumza ila nikajikuta nikishindwa kabisa na nikaanza kutembea kuelekea ofisini kwanbu na kumfanya Martin kunifwata kwa nyuma, kabla sijafika kwenye mlango wa ofisini Martin akanishika bega langu la upande wa kulia na kujikuta nikisimama.

“Mkuu mimi ni msaidizi wako”   

“Nimekuelewa Martin nitakuambia badae sawa”

“Sawa mkuu”

Nikafungua mlango na kuingia ndani, nikamkuta Yemi akiwa hayupo. Ikanibidi kutoka tena ofisini kwangu.

“Vipi mkuu?”   

“Mke wangu hayupo?”

“Labda atakuwa amerudi ndani?”

 

Tukaanza kuongozana na Martin hadi kwenye nyumba ninayo ishi, nikaingia chumbani kwangu na kumuacha Martin sebleni. Sikumkuta Yemi zaidi ya nguo zake zikiwa kitandani, nikasikia maji yakimwagika bafuni, nikajikuta nikianza kutembea taratibu hadi bafuni, nikafungua mlango wa bafuni, cha kushangaza sikumkuta Yemi, zaidi ya maji ya bomba la mvua yanayo mwagika. Kwa haraka nikafunga bomba hili la maji na kutoka hadi sebleni.

“Mke wangu hayupo ndani”

Nilizungumza huku mapigo ya moyo yakinienda kasi kwani, nimesha anaza kupata hisia mbaya hukusiana na kutoweka kwa Yemi ambaye alisha niahidi kwamba hii vita ni lazima ataiingilia.

 

Waambie wanajeshi wote kwamba mke wangu hayupo wahakikishe wanamtafuta ndani ya hii kambi sawa”

“Sawa jenero”

Martin akatoka kwa kasi humu ndani na kuniacha sebleni nikiwa nimechanganyikiwa. Nikarudi chumbani tena, katika kutazama tazama juu ya meza nikaona karatasi nyeupe kwa haraka nikaichukua na kukuta maandishi yaliyo andikwa kwa kalamu ya wino mweusi.

‘Mume wangu Dany/Peter, natambua kwamba haya ni maamuzi magumu niliyo yachukua ila nimefanya hivi kwa sababu ninakupenda mume wangu. Sihitaji kuona damu yako inamwagika kwa ajili ya mtoto ambaye sio damu yako. Natambua kwamba unanipenda na unanijali ila nimejitolea maisha yangu kwa ajili ya jambo hilo. Ninakuomba sana unisamehe mume wangu. Kwaheri’

 

Nikajikuta nikifinyanga finyanga karatasi hii kwa nguvu huku nikilia kwa uchungu mkubwa sana. Nikajifuta machozi yangu usoni kisha nikaanza kutembea kuelekea nje huku hasiri niliyo nayo sijawahi kuipata tangu kuzaliwa kwangu.

“Mkuu”   

Niliisikia sauti ya meja akiniita huku akiingia kwenye mlango wa kuingilia hapa sebleni. Kwa macho niliyo mtazama nikamuona meja akikaa kimya kwa sekunde kadhaa. Sikuzungumza kitu chochote zaidi ya kumtazama usoni mwake.

 

“Nimesikia mke wako ametoweka?”       

Nikamkabidhi meja karatasi niliyo ifinyanga, akaifungua taratibu na kuanza kuisoma, nikamuona meja akishika kichwa chake huku akionekana kupatwa na mshangao mkubwa sana.

“Waambie wahakikishe kwamba wanamleta mke wangu hapa. Kwa garama ya aina yoyote ninamuhitaji mke wangu”

“Sawa mkuu nitahakikisha kwamba mke wako  hatoke ndani ya nchi hii ni lazima tumrudishe hapa”

Martin akaingia na kutufanya mimi na meja kumtazama.

“Mkuu nina habari mbaya”

“Habari gani?”

Martin akanikabidhi simu yake nikaanza kuiona video inayo muonyesha Yemi akijisalimisha mikononi mwa wanajeshi wa kimarekani, akishuka kwenye helicopter ambayo ina chata la jeshi langu.

 

“Aliiba helicopter moja na kuondoka nayo”

Nikajikuta nikipepesuka huku miguu ikiniishiwa na nguvu kabisa. Martin na meja wakaniwahi kunishika na kwa haraka wakanikalisha kwenye sofa. Macho yangu yakaanza kububujikwa na machozi huku nikiitazama video hii iliyo chukuliwa na simu, nikawaona wanajeshi Wakimarekani jinsi wanavyo mvisha pingu Yemi.

“Amejisalimisha kwenye kambi ndogo ya jeshi iliyopo hapa nchini Nigeria”

Martin alizungumza huku akinitazama usoni mwangu. Kwa ishara meja akamuomba Martin asizungumze chochote kwani akili yangu kwa sasa haipo vizuri. Nikairudia tena kuitazama video hii nikashusha pumzi nyingi huku nikijitahidi kuizuia hii hali ya kupoteza nguvu mwilini mwangu. Nikaka zaidi ya dakika kumi nikiitazama hii video. Taratibu nikasimama wima, nikamkabidhi Martin simu yake.

“Kambi ipo wapi?”

“Abuja”

“Niandalieni vikosi kabla hawajamsafirisha mke wangu kumpeleka Marekani”

“Ila mkuu unaweza kuwa ni mtego wa kuhitaji kukupata wewe kirahisi”

“Meja unataka kuniambia kwamba mke wangu ni msaliti si ndio?”

“Hapana jenero”

“Ila…”

“Nimekushauri tu mkuu, kwa maana lengo la Wamarekani wanakuitaji wewe”

“Wakinikamata basi ila ninahitaji muandae vijana, nipeleke kwenye ghala la silaha”

“Sawa mkuu”

 

Martin alizungumza na kuanza kunifwata kwa nyuma, meja naye akaanza kutufwata.

“Jenero nina imani kwamba ushauri wangu kwa muda mwengine unakwenda tofauti na maamuzi yako, ila ningekuomba hili tuweze kulifikiria mara mbili mbili. Ninaimi hii ni njia rahisi sana Wamarekanani wanaweza kuitumia kupata wewe ukitegemea kwamba wewe ndio mkuu wa hili kundi hili. Ukiondoka unahisi ni nani atakaye ongoza hili jeshi?”

“Wewe ndio utaongoza”

“Jenero umri wangu kwa sasa umekwenda, nimesha kuwa mzee sana, muda wowote ninaweza kuondoka duniani, jeshi linahitaji vijana ambao ndio nyinyi. Tafadhali ninakuomba niandae kikosi cha kwenda kumuokoa mke wako”

“Meja una mke?”

Nilimuuliza meja huku nikisimama na kumtazama usoni mwake kwa hasiria. Taratibu meja akajibu kwa kutingisha kichwa chake.

“Unajua uchungu wa mke?”

“Hapana mkuu”

 

“Kaa kimya katika hili, hili ni tataizo la kifamilia na si tatizo la jeshi lako ninacho kiangalia hapa ni mke wangu kuwa salama sawa meja?”

“Nimekuelewa mkuu samahani kwa ushauri wangu kwako”

“Ninakuomba uniandalie wanajeshi wanne, ninakwenda kuivamia hiyo kambi ya Wamarekani”

“Wanajehshi wanne?”

“Ndio”

Meja akatazamana na Martin, kisha meja akaondoka eneo hili. Nikaanza kutembea kuelea kwenye ghala la kuhifadhia silaha pamoja na nguo za kijeshi. Tukaingia kwenye ghala hili ambalo linalindwa sana na wanajeshi kwani hapa ndipo kwenye silaha zote za kundi hili. Wanajeshi wote wakanipigia saluti huku wakisimama kikamavu.

“Nahitaji nguo zitakazo nitosha mimi”

“Zipo  meja”

Nilimuambia mmoja wa watunzaji wa nguo katika ghala hili. Nikaingia katika ukumbi wa kuhifadhia silaha, nikaanza kuchukua bastola mbazo ninaimani zitanisaidia katika kupambana kwangu. Martin naye nikamuona yupo katika harakati ya kuchukua silaha zinazo mfaa yeye.

 

“Unafanya nini Martin?”

“Mkuu ninahitaji kwenda na wewe”

“Martin hii vita itakuingiza kwenye matatizo”

“Mkuu najua upo juu yangu ila hili sio ombi kwako. Ninaifanya kazi ambayo umenikabidhi nitahakikisha kwamba ninakwenda na wewe sehemu yoyote utakapo kuwa, iwe kwenye shida ama raha ni lazima niwe na wewe jenero”

Nikamtazama Martin usoni mwake, sikuhitaki kumzuia, tukaendelea kuandaa silaha zetu. Nikamuona Martin mara kwa mara akiwa ameweka mkono wake wa kushoto kwenye sikio lake la upande wa kushoto.

“Una kinasa sauti cha nini?”

Swali langu likamfanya Martin kustuka na kubaki akinitizama kwa maana nina ujuzi sana na mtu aliye vaa kinasa sauti sikioni kwani walinzi wote mara nyingi huvaa vinasa sauti kwenye masikio yao ili kuhakikisha kwamba wanapena taarifa zozote zinazo endelea katika eneo ambalo wapo.

“Mkuu nilimuweka meja kinasa sauti kwenye mfuko wa koti lake la jeshi ili kila mazungumzo yenu munayo yazungumza nipate kuyasikia kwani nilihitaji kufahamu ni kitu gani kinacho endelea”

 

“Kwa hiyo una tupeleleza?”

“Hapana mkuu, nimefanya hivi kwa ajili ya usalama wako, kumbuka mimi kwa sasa ndio mtu wako wa karibu pasipo kufanya hivi nitakuwa nipo nyuma ya muda na maamuzi ya kuhakikisha kwamab mkuu wangu unakuwa salama”

Nikamtazama Martin usoni mwake, nikamuona Martin akiongeza usikivu katika kusikiliza.

“Nini?”

“Mkuu unatakiwa kusikia hichi”

Martin akavua kinasa sauti chake na kunikabidhi mimi, nikakivaa katika sikio la upande wa kulia.

‘Hakikisheni kwamba jenero haendi popote, ikiwezekana hata kwa kumchezea rafu ya kumchoma sindano ya usingizi. Sawa?’

Niliisikia sauti ya meja ninaimani anazungumza na wanajeshi ambao nimempa kazi ya kuniandalia

‘Sawa mkuu ila hili ni hatari sana na endapo jenero akijua ninaimani kama alivyo sema atatuua kwa mana sisi tutakuwa ni wasaliti wa amri yake.’

 

‘Kwani kuna mmoja wenu ambaye anaweza kuitoa hii siri?’

‘Hakuna meja, sisi ni vijana wako’   

‘Sawa fanyeni hivyo, yote ninafanya kwa ajili ya kumlinda jenro sihitaji aondoke kwenda popote, kwani bado tunamuhitaji kwenye hili jeshi’

‘Sawa mkuu’

Nikavua kinasa sauti hichi huku nikiwa nimejawa na gadhabu kubwa sana kwani meja anajaribu kunizuia kwa kile ambacho nimekiamua na hafahamu ni ukweli gani ulipo katikati ya hili tatizo ambalo pasipo kuwa makini litayagarimu maisha ya watu wengi wasio na hatia ikiwa mimi mwenyewe ninaweza kulishuhulikia na kulimaliza hata kama ni kwa kupoteza maisha yangu ila litakuwa limeisha nahalito endelea kwenye uso wa dunia.





“Tutakwenda peke yetu”

Nilizungumza huku  nikimtazama Martin usoni mwake.

“Mkuu sa…..”       

“Hawa ambao meja ananiletea ni wasaliti katika hili swala na hakuna hata mmoja anaye tambua ni kity gani kinacho endekea kati tangu na Marekani. Sinto hitaji msaadawa wa mtu mwengine zaidi yako sawa?”

 

“Sawa mkuu”

Tukamaliza kujiandaa, meja akaingia huku akiwa ameongozana na watu nilio muomba aweze kunichagulia na kuniletea.

“Mkuu vijana hawa hapa wamekamilika kila idara unaweza kwenda nao”

Nikamtazama meja kisha nikawatazama vijana hawa kwa macho makali hadi wakajistukia na kuanza kutazamana. Nikachukua bastola moja iliyopo juu ya meza, nikaikoki vizuri na kmnyooshea mmoja wa kijana huku macho yangu nikiendelea kumkazia.

“Unaweza kufanya alicho kuambia meja wako?”

Kijana huyu akaanza kutetemeka mwili wake wote. Nikaielekezea kwa kijana mwengine huku naye nikiwa nimemkazia macho.

“Unaweza kufanya alicho kuagiza meja kukifanya?”

Kijana huyu naye hakunijibu kitu chochote zaidi ya kukaa kimya huku akinitazama.

“Meja, hili ulio lifanya leo siku nyingine ukirudi nitakuchukulia hatua za kisheria kali, Tumeelewana?”

“Mkuu sijakuelewa unamaanisha nini?”

Nikamsogelea meja nikaingiza mkono kwenye mfuko wa kulia wa koti lake sikukuta kitu chochote, nikaingiza kakatika mfuko wa upande kushoto, nikatoa kifaa kidogo ambacho ni kinasa sauti, nikamkabidhi mkononi mwakae na kumfanya meja kushangaa sana.

“Meja kumbuka maisha yangu na uongozi wagu ninatumia akili, unapo fanya vitu na wewe tumia akili sana kwa maana siku nyinine utafeli sawa. Hawa vijana wako siwahitaji kwenye opareheni hii, nitakwenda na Martin sisi wawili na tutajua ni nini cha kufanya”

 

“Samahani sana jenero kusudio langu halikuwa baya sana kwenye hili swala”

“Natambua ila unatakiwa kusirikiza amri ya mkuu wako na si kupinga amri yake hata kama kuna faida nzuri itapatikana kwa kuzuia amri yake”

“Sawa jenero”

Tukabeba kila tulicho kusudia kukibeba na Matrin, tukaelekea katika uwanja wa helicopter.

“Tunahitaji rubani?”   

“Hakuna haja mkuu, ninajua kuendesha helicopter”

Martin alizungumza huku akifungua mlango wa helicopter moja, tukaingia ndani, sikuhitaki kubisha. Taratibua Martin akaanza kuwasha helicopter hii ambayo haikuchukua muda mrefu sana ikashika kasi katika banka lake. Martin taratibu akaanza kuinyanyua helicopter hii kwenda juu.

“Mkuu vaa hizo earphone”

Martin alizungumza huku akinionyesha earphone kubwa zilizopo pembeni yangu, nikazichukua na kuzivaa masikioni mwangu, huku na yeye akivaa earphone zinazo fanana na hizi.

“Hapa tunaweza kuwasiliana na watu walipo  kambini?”

“Sawa sawa”

“Mkuu inabidi kuomba muongozo wa watu walipo chumba cha mawasiliano ili iwe rahisi kwa sisi kuweza kuivamia kambi hiyo”

“Unafahamu ilipo kambi?”

“Ndio ninaifahamu ila itakuwani kambi ambayo ina ulinzi mkali sana ambao unaweza kutukamata mapema sana”

“Wasiliana na watu wa chumba cha mawasiliano”

“Sawa”

“Mia moja kumi na moja, Erick ninazungumza hapa”

“Ndio tunakupata Erick?”

“Nipo na jenero Peter tunaomba msaada wa kuweza kuingia katika kambi ya Wamarekani”

“Nimesha weza kuhaki mfumo mzima wa ulinzi wa kamera katika kambi hiyo na kila kitu kinacho endelea kwenye hiyo kambi tunakiona”

 

“Vipi mke wangu yupo?”

“Ndio mkuu mke wako bado yupo kwenye hiyo kambi”

“Naomba muhakikishe kwamba munanieleza kila kitu ambacho kinacho endelea katika kambi hiyo sisi tukiwa njiani”

“Sawa mkuu, yupo kwenye moja ya chumba, na tunaweza kutumia njia ya chini ya ardhi kuweza kufika katika chumba hicho”

“Hiyo njia ipo wapi?”

“Mita mia tisa kabla ya kufika kwenye kambi hiyo”

“Ila mita mia tisa ni nyingi sana na tukishuka kwenye helicopter hii si tutapoteza mawasiano nanyi”

“Ndio mkuu hiyo ndio nyia rahisi ya nyinyi kuingia katika kambi hiyo na kumkomboa mke wako”

Nikaka kimya huku nikitafakari kitu cha kufanya.

“Mkuu”   

“Tuelekezeni hiyo sehemu ipo wapi?”

“Ni kwenye moja ya mnara wa simu, pembeni yake kuna mfuniko wa chuma mukiingia humo munaweza kuingia na kwenda moja kwa moja hadi kwenye sehemu kilipo chumba hicho.

 

“Sawa nimekuelewa, meja yupo humo ndani?”

“Ndio jenero nipo?”

“Tofauti tuziweke pembeni, ninahitaji kikosi kitakacho kuja nyuma yangu, na ninahitaji kikosi cha anga ninahitaji kuiteketeza hiyo kambi nzima”

“Sawa mkuu nimekuelewa nitaanzaa vikosi viwili, kikosi cha anga na kikosi cha ardhini”

“Shukrani, Martin unafahamu sehemu ulipo huo mnara?”

“Ndio ninafahamu muheshimiwa”

“Sawa fanya hivyo”

Tukatumia dakika kama dakika kumi na tano kufika katika mnara wa simu tulio elekezwa, taratibu Martin akaitulisha hii helicopter hii. Akaizima, kisha tukashuka kwenye hii helicopter. Haikutuchukua muda kuupata mfuniko huu  wa chumba, taratibu tukashirikiana kuufungua kwa maana ni mzito sana.

 

Martin akatoa kitochi kidogo na kumulika ndani kwa maana kuna giza, tukaona ngazi za chuma zinazo elekea chini, Martin akawa wa kwanza kushuka kisha nikafwatia mimi kushuka, tukaanza kutembea kuelekea mbele kwa kutia mwanga mdogo wa hii tochi.

   Tukazidi kusonga mbele kila mmoja akiwa ameshika bastola yake mkononi, ikatuchukua zaidi ya nusu saa tukawa tumefika kwenye sehemu ambayo tumekuya ngazi za kuelekea juu. Taratibu Martin akaanza kutembea kupandisha ngazi hizo hadi tukafanikiwa kufika juu ambapo napo kuna mfuniko.

“Vipi?”

“Ni mzito kama ule wa kule”

“Duu sasa tunaweza kuufungua?”

“Huu ubara wake ni kwamba umefungwa kwa nati na ili kuufungua ni lazima mtu uwe kwa juu”

“Mmmm kwa hiyo kazi yote tuliyo ifanya ni bure?”

“Hapana mkuu tunaweza kuvunja hili eneo kwa kutumia bomu la kutega”

“Ila si umeambiwa kwamba mke wangu yupo kwenye hicho chumba hapo juu”

 

“Ndio mkuu ila hatuna jinsi ya kufanya zaidi ya kufanya hivyo”

Martin akashuka kwenye ngazi na kusubiria jibu langu ili apande kuweka bomu ambalo litakwenda kuchangua eneo hili la mfuniko.

“Mkuu hiyo ndio njia ya pekee ambayo tumebakiwa nayo”

“Weka bomu”

Martin akafungua begi tulilo hifahidhia baadhi ya mabomu, akatoa bomu moja, akatega dakika tano, kisha akapanda kwa haraka na kulitega sehemu ambayo kuna mfuniko, akashuka na tukaanza kukimbia kurudi sehemu tulipo tokea kwani mlipuko wake unaweza ukawa ni mkubwa. Tulipo fika umbali ambao tukahisi kwamba mlipuko huo hautoweza kutuathiri, tukasimama. Mlipuko mzito ukatoke katike ene hilo na vipande vizito vizito vya matofali vikaangukia humu ndani. Tukaanza kurudi eneo hilo huku tukikimbia kwa kasi. Kwa haraka Martin akapanda kwenye kifusi hichi cha matofali yaliyo angukia humu ndani, akafanikiwa kufika kutoa juu. Na mimi kwa haraka nikapanda kwenye kifusi hichi na kutokea katika chumba ambacho tulitarajia kumkuta Yemi ila hatujampata kabisa.

 

“Hayumo humu?”

Nilizungumza huku nikisikilizia ving’ora vya tahadhari vinavyo endelea kulia katika eneo hili. Nikaufungua mlango wa chumba hichi na kuchungulia nje nikakuta wanajeshi wangi wakikimbia kwa kasi wakija katika hii kordo.

Kwa haraka nikaanza kuwashambulia kwa risasi, kwani hii ndio njia ya pekee ya sisi kuwazuia wanajeshi hawa. Tukaanza kupeana zamu na Martin katika kuwashambulia wanajeshi hawa.

“Naomba Granade”

Nilizungumza huku nikiwa nimejibaza, Martin akachomoa bomu la mkono ambalo ameninginiza kwenye mkanda wa kiunoni mwake. Akanikabidhi bomu hilo, nikachomoa kipini cha bomu hilo na kulirusha sehemu walipo jificha wanajeshi hawa, na kusabisha mlipuko mkubwa.

“Tutoke humu”

Nilizungumza huku nikianza kutoka kwenye hichi chumba na kuanza kusonga mbele kuhakikisha kwamba tunatafuta ni sehemu gani alipo Yemi. Mashambulizi ndani ya hili jengo yakazidi kupamba moto kwani kadri muda ulivyo zidi kwenda ndivyo jinsi tulivyo kutana na wanajeshi ambao wanazidi  kuongezeka kuhakikisha kwmba hatutoke ndani ya kambi yao.

“Mkuu”

“Ndio”

“Risasi zimeniishia”

Martin alizungumza huku akinitazama na kujikuta nikimtazama huku macho yakinitoka, nikajipapasa kwenye mfuko wangu na kukuta nina magazine moja tu. Nikachomoa magazine iliyopo kwenye bastola yangu nikakuta nayo ina risasi nne zilizo salia na mbaya wanajeshi wanzidi kumiminika na sehemu tuliyo jificha kusema kweli wakiamua kurusha bomu la mkono tunakufa.

“Hakikisheni tunawakamata wazima”

Nilisikia sauti ya mmoja wa wakuu wa hili jeshi, hapo ndipo nikafahamu kwamba kazi imezidi kuwa ngumu kwetu.

“Dany tunajua upo hapa, na umekuja kumuokoa mke wako. Jisalimishe mikononi mwetu la sivyo tunamuua mke wako”

“Dany!!?”

Martin aliniuliza kwa mshangao huku akinitazama usonim wangu.

“Ni jina langu usishangae”

“Ila mkuu huwezi kujisalimisha kirahisi namna hii?”

“Inabidi kufanya hivi, nikijisalimisha mchukue mke wangu na kuondoka naye sawa”

“Mkuu jukumu langu ni kukulinda hadi mwisho wa maisha yangu, tutakufa pamoja”

 

“Martin hili sio ombi ni amri sawa, ninajisalimisha mchukue mke wangu na uondoke naye hapa na lengo langu kubwa kuja hapa ni kujisalimisha kumalizana na hili jambo linalo jitokeza hapa”

“Mkuu hapana”

Martin alizungumza huku akiniomba magazine yangu ya risasi.

“Hatuwezi kutoka humu ndani Martin na sipendi ubishane na amri yangu”

“Kwa nini wanakutaka wewe?”

“Nilikuwa ni mpelelezi wa Kimarekanai, wamenisaliti na nikaamua kuwasaliti. Ila huu sio muda wa kupiga story ninakuomba mke wangu mchukue na kuondoka naye hili eneo”

Martin hakuwa na jambo la kujibu zaidi ya kukaa kimya.

“Ninahitaji kumsikia mke wangu kwanza”

Nilizungumza kwa sauti ya juu huku nikiendelea kujibanza kwenye hili eneo.

“Dany usitoke mume wangu”

Niliisikia saauti ya Yemi akizungumza huku akilia.

“Yemi”

“Ndio mume wangu kwa nini umenifwata jamani”

“Usijali mke wangu. Ninahitaji mumuachie mke wangu na ninajitokeza”

 

Nilizungumza huku nikimkabidhi Martin magazine iliyo salia, kisha taratibu nikanyanyuka kutoka katika eneo hili niliko jificha huku bastola yangu nikiwa nimeinyoosha kwa juu. Nikamuona Yemi akiwa amehishikiliwa na wanajeshi hawa wa Kimarekanani ambao idadi yao kwa haraka haraka inaweza kufika mia moja.

“Muachieni mke wangu, nipo tayari kujisalimisha mikononi mwenu”

Taratibu wakamuachi Yemi aliye anza kutembea kwa mwendo wa taratibu akija eneo hili nilipo, na mimi nikaanza kutembea kwa mwendo wa taratibu huku nikiwatazama wanajeshi hawa walio ninyooshea mitutu ya bunduki zao na endapo nitafanya kosa lilote wataniua mimi na Yemi jambo ambalo sihitaji litoke mbele ya macho yangu.



Tukakutana na Yemi katikati, akanitazama usoni mwangu huku machozi yakimwagika.

“Nenda”

Nilizungumza kwa sauti ya upole iliyo jaa simanzi ndani yake.

“Kwani nini umefanya hivi mume wangu?”

“Hakuna jinsi ya kufanya mke wangu nenda, nenda tafadhali”

Niliendelea kuzungumza kwa huzuni ila kwa msisitizo kidogo, Yemi hakuwa na ubishi zaidi ya kuazidi kusonga mbele hadi sehemua lipo jificha Martin. Nikasimama futi sita kutoka alipo simama mkuu huyu wa jeshi.

“Muacheni mke wangu na mlinzi wangu waondoke hili eneo”

“Usijali hatuwezi kuwagusa”

“Niahidini?”

“Waruhusu waondoke”

“Martin ondoka na shemeji yako”

Nilizungumza kwa sauti ya juu, nikageuka nyuma nikamuona Martin akinyanyuka sehemu hiyo, akamshika Yemi mkono aliye zidisha kulia kwa uchungu kwani ninaimani kwamba hawezi kwenda kuniona tena kwenye maisha yake.

“DANYYYYYYYYY”

Yemi alilia kwa uchungu sana huku Martina akiw ana kazi ya kumkimbiza kuelekea katika chumba tulicho ingilia. Nilipo hakikisha wameingia kwenye chumba hicho nikageuka mbele na kumtazama mkuu huyu wa jeshi. Wakaichukua bastola yangu na kunifunga pingu, za mikononi pamoja na nyororo ngumu na ndefu kiasi kwenye miguu yangu. Wanajeshi hawa wakaanza kunikimbiza mkuku mkuku hadi kwenye moja ya ndege ya kijeshi, wakangiza huku nikiwa katika ulinzi mkali sana. Wakaniingiza katika chumba kilicho tengenezwa na nondo ngumu, kisha wakakinga kwa nje. Mkuu wao akanisogelea huku akiwa ameshika simu mkononi mwake.

“Muheshimiwa raisi nimeweza kumpata Dany”

Nikasoma jina la mkuu huyu kwenye mfuko wa shati lake na kugundua kwamba anaitwa Josephat D.R

“Kama ulivvyo niagiza mkuu wangu, nitahakikisha ninamfikisha Marekani baada ya masaa machache na mke wake nimeagiza vijana wanakwenda kumuua na hawawezi kutoka mikononi mwetu”

Nilitamani kukata pingu hizi kwa hasira ila sina uwezo wala nguvu ya kufanya hivyo kwani sikutegemea kwamba hawa jamaa wanaweza kunisaliti na kwenda kinyume na makubaliano ambayo tumeyaweka kuhusiana na mke wangu pamoja na mlinzi wangu ambaye nina imani kwamba nimemuacha katika mazingira magumu sana.

“Malaya mkubwa wewe”

Nilijikuta nikitukana kwa hasira na kumfanya mkuu huyu kucheka kwa kejeli. Akaondoka huku simu yake akiwa ameishika mkononi mwake na ninaimani kwamba alikuwa anarekodi video. Ndege hii ya kijeshi ambayo ipo tofauti kabisa na ndege za abiria, kwani haina siti hata moja. Wanajeshi wakakaka kwenye mizigo iliyopo humu ndani, na taratibu ndege hii ikafungwa na nikasikia mlio wa injini ya ndege hii zikianza kuwashwa.

Moyoni mwangu nikajikuta nikianza kujilaumu kwa kuweza kufanya maamuzi ya kujiamini na kushindwa kumsikiliza meja ambaye kwa haraka haraka ni sawa na baba yangu. Hadi sasa hivi wala sielewi wanajeshi wangu wa Boko haramu wamekwamia wapi kwani hadi sasa hivi sijasikia shambulizi hata moja.

Hadi ndege ikapaa hewani hapa ndipo nikajikuta nikikata tamaa kabisa. Taratibu nikajikuta nikikaa chini huku machozi ya hasira yakinimiminika usoni mwangu. Sijajua kifo changu kinakwenda kuwa cha aina gani, kwani ni nimeweza kuwaua wanajeshi wengi wa Marekani hususani makomandoo wao ambao  waliwaagiza kwa ajili ya kunisaka mimi.

“Kazi nzuri”

Nilimsikia meja akizungumza na simu yake ya mkononi. Akasimama na kunisogelea sehemu nilipo.

“Una habari?”

Aliniuliza kwa dharau huku akiwa ameinama, nikanyanyua uso wangu na kumtazama huku nikizidi kujawa na hasira.

“Kambi yako ya boko Haramu hadi sasa hivi ipo PUUUUUUUUUUUUU……!!”               

Maneno ya mwanajeshi huyu yakanifanya nisimame kwa haraka huku nikiwa nimeshikwa na mshangao mkubwa kwani kuondoka kwangu ninaimani kwamba kumeleta matatizo makubwa sana.

“Sasa hivi hakuna Boko Haramu, wala Boko njemaaa. Umepoteza Dany, wewe anza kusali sala yako ya mwisho kwani ukifika Marekani ni kunyongwaaaaa tuu”

“Krgahaaaaaaaaaaaaaaaa”

Nililia kwa hasira huku nikijaribu kuitoa mikono yangu nje ya hizi nondo huli nijaribu kumshika mkuu huyu wa jeshi hili la Wamarekani, ila sikuweza kumshika na alicho kifanya ni kurudi nyuma yangu kwa hatua chake akaviweka vidole vyake gumba kichwani mwake na kuchezesha vidole vyake vilivyo salia huku ulimi wake akiutoa nje, ishara ambayo ni kejeli kubwa sana juu yangu na ananizomea kwa kunidharau.

“Dany huna cha kufanya sasa, umefuliaa baba”

“Siwezi kufa kabla sijalipiza kisasi kwa wale walio nifanyia mabaya. Usijiingize kwenye vita ambayo haikuhusu kwa mana utakufa pasipo sababu ya msingi”

Nilizungumza kwa sauti nzito sana huku nikimtazama mwanajeshi huyu, akazungumza neno moja ambalo sikulielewa na kuwafanya wanajeshi wake wote kucheka kwa dharau sana.

“Huna njia ya kutokea Dany, tena muheshimiwa raisi anakusubiria kwa hamu sana”

“Nashukuru”

Nilijibu kwa upole wa kuigiza ila moyomi mwangu nimejawa na hasira moja kali sana. Mkuu wao huyu akarudi sehemu yake, akafungua begi dogo, akatoa laptop na kurudi sehemu nilipo, akafungua laptop hii na kuanza kuminya minya batani zake.

“Ninawasiliana na raisi moja kwamoja nina imani atafurahi kukutana na wewe”

Jamaa alizungumza huku akiwa ameishika laptop. Baada ya kufanya anacho kifanya akageuza laptop ussawa wangu huku akiwa amesimama mbele yangu. Nikamona raisi bwana Donald Bush akiwa amekaa kwenye kiti chake cha uraisi

“Muheshimiwa raisi nilihiji kukutumia video kukuambia kwamba nimemkamata Dany ila nikaona tuwasiliane moja kwa moja tukiwa tunaonana”

“Waoooo nimemuona, habari yako Dany”

“Mkuu pia nina habari mpya”

“Niambie tu”

Raisi alizungumza huku  akiwa amejawa na furaha sana.

“Hadi ninavyo zungumza hivi sasa ni kwamba kambi ya Boko Haramu imefumuliwa kisawa sawa na wanajeshi wetu”

“Kweli?”

“Ndio muheshimiwa raisi japo sijapata ripoti ya kukamatwa kwa mke wake”

“Ila vijana si uliwaagiza?”

“Ndio niliwagiza”

“Kwa sasa nipo kwenye Air Foce One ninaelekea Urusi hakikisheni mukimfikisha Marekani munamueka chini ya ulinzi hadi nitakapo rudi.”

“Sawa sawa mkuu”

“Ngoja mara moja, mke wangu njoo hapa uone kitu”

Nikaiona sura ya Hawa, ambaye baada ya kuniona mimi akaonekana kushangaa sana na kustuka. Raisi akambusu Hawa shavuni mwake.

“Nakupenda sana mke wangu”

“Ninakupenda pia mke wangu”

“Sajenti tutaonana Marekani baada ya siku mbili”

“Shukranu muheshimiwa raisi”

Mawasiliano haya kwa njia ya video kati ya raisi Donald Bush pamoja na Sajent Josephat yakaishia hapo, akaifunga laptop yake na kurudi kukaa kwenye sehemua lipo kuwa amekaa huku akiwa na tanasamu pana sana.                       

‘Lazima niwaue wote’

Nilizungumza hukku nikiwatazama wajeshi hawa kwa macho makali sana. Masaa yakazidi kusonga mbele, gafla kitu kizito kikasikika kikiipiga hii ndege na kuifanya kuyumba. Wanajeshi walio jiegesha kupata usingizi wakajikuta wakikurupuka kutoka kwenye usingizi.

Wanajeshi wote wakajikuta wakishika bunduki zao na kuwa makini sana. Hadi sasa hivi sielewi ni kitu gani kinacho endelea. Kishindo kingine kikasikika na hichi kikashinda hata kishindo cha kwanza. Mlango wa pembeni wa hii ndege ukang’ofolewa na kusababisha upepo mwingi sana kuingia ndani ya hii ndege. Wanajeshi ambao wamesimama kizembe zembe walijikuta wakivutwa nje na upepo huu amba una nguvu kubwa sana.

“Fungeni mikanda haraka”

Sajenti alizungumza na kuwafanya wanajeshi wengine wanao pambana kukaa vizuri kuwenye viti vyao kuhakikisha kwamba wanaifunga mikanda ya sehemu walizo kali.

Gafla hali ya hawa ndani ya hii ndege ikazidi kuwa nzito hii ni baada ya kuingizwa bomu dogo la gesi inayo fanya watu kumwagikwa na machozi. Ukungu mwingi ukatawala ndani ya hii ndege, nikasikia milio ya risasi na vilio vya wanajeshi wa Kimarekani hadi mimi mwenyewe nikajikuta nikichangayikiwa kwani hili shambulizi hadi sasa hivi sijui limefanywa na nani.

“Huyu hapa”

Nilisikia watu wakizungumza, kufuli nje ya kibanda hichi cha chumba likavunjwa kwa kupigwa risasi kadhaa. Kwa haraka nikavalishwa kifaa maalumu kichwani kwangu cha kuzuia kuivuta gesi hii ambayo inamnyong’onyeza mtu.

“Jenero Peter”

Mtu huyu anaye sumbuka kunifungua pingu za mikoni alizungumza

“Ndio ndio”

“Upo salama muheshimiwa”

Jamaa huyu akafanikiwa kufungua pingu za mikono yangu, kisha akafungu mnyororo nilio  fungwa miguuni mwangu.

“Ongozana nasi muheshimiwa”

“Nyinyi ni kina nani?”

Niliuliza kwa sauti ya juu kwa maana upepeo unao zidi kuingia ndani ya hii ndege unazimeza saiti zrtu kiraisi sana.

“Utanifahamu tu jenero, ongozana nami”

“Samahani ninaomba silaha yako”

Jamaa huyu bila ya kipingamizi akanikabidhi bastola yake, taratibu nikajikaza kutembea huku mku mkono moja nikishika sehemu ili nisianguke, nikafika hadi sehemu alipo kaa Sajenti Josephat, nikamkuta akiwa anaugulia maumivu ya risasi alizo pigwa mguuni mwake.

“Nilikuambiaa nitatokaa”

Nilizungumza huku nikimtazama jinsi anavyo pata shida ya kuupelekea mkono wake kwenye bastola yake iliyo angukia pembeni, ila hana ngungu ya kufanya hivyo.

“Nisalimie huko ulipo kuwa unahitaji kunipelekea”

“Malay……….”

Hakumalizia sentensi yake nikampiga risasi mbili za kichwa kisha nikamrudishia jamaa huyu batola yake, kisha akaniomba nisimame mbele yake akanikimbatia kwa nguvu na kujikunga mkanda ulio tufunga viunoni mwetu, akanikabidhi.

“Jenero nishikilie kisawa sawa”   

“Sawa”

“Moja, mbili, tatu”

Jamaa huyu akaruka pamoja na mimi, huku wezake wawil walitufwatia kwa nyuma. Tukaanza kwenda chini huku tumetanguliza vichwa vyetu jambo lililo niongopesa sana, ila nikajikausha kimya nisionekane muoga sana kwani mchezo huu ni mara ya pili sasa unajirudia kwenye maisha yangu na mara ya kwanza nilifanya nikiwa katika opareheni ya kwenda kuvamia kundi la Al-Shabab nchini Somalia.

Jama huyu wala sikujua amefanya nini, tukajikuta tumegeuka tu na kuanza kuanguliza miguu yetu, nikaanza kuona ndege nyingine ikiwa chini yetu.

“Tunatua juu ya hiyo ndege iandae miguu yako jenero”

Jamaa huyu alizungumza, na kujikuta nikijianda kwa tukio hili ambalo litatokea baada ya muda mfupi sana. Tukatua juu ya ndege hii, japo kuna upepo mwingi sana, ila huyu jamaa nina imani ana mafunzo makubwa sana kwenye hili analo lifanya, laiti kama ningekuwa peke yangu basi ni muda mwini sana ningekuwa nimesha kufa. 


Wezake wawili nao wakatua juu ya hii ndege inayo endelea kwenda. Kuna sehemu mbele yetu ikafunguka taratibu na tukaingia kwa pamoja ndani ya hii ndege huku jamaa hawa wawili wakifwatia na sehemu hii ikajifunga. Jaamaa akafungua mkanda alio nifunga kiunoni mwangu, kisha akavuaa vifaa maalumu vya kuzuia gesi. Nikabaki nikiwashangaa kwani wana asili ya Kimarekani. Nikavua na mimi huku nikiendelea kuwashangaa.

“Tunaomba utufwate”

Nikaanza kuwafwata huku tukitembea kwenye kordo ndefu ya hii ndege inayo onekena ni ya kifahari kwa maana hakuna hata abiri mmoja zaidi ya wahudumu wakike. Tukaingia kwenye moja ya chumba sikuamini macho yangu baada ya kukutana na meja wa Kimarekani ambaye alitokea kunipenda sana kwa kipindi nilipo kuwa kambini kwake nchini Somalia.



“Meja”   

“Karibu sana rafiki yangu Dany”

“Asante sana meja”

Nilijikuta nikizungumza huku furaha kubw aikiwa imenitawala sana usoni mwangu. Tukakumbatia kwa sekunde kadhaa kisha tukaachiana.

“Pole sana kwa matatizo yaliyo kupata”

“Nashukuru sana”

“Naombeni mutuachie chumba”

Meja akawaambia wanajeshi wake hawa, wakatoka ndani ya chumba hichi na kutuacha wawili. Meja akanikaribisha kukaa kwenye sofa lilipo pembeni yangu.

“Mke wako pamoja na mlinzi wako hadi sasa ninavyo zungumza wapo salama”

“Kweli meja?”

“Asilimia mia moja na kwa sasa wapo kwenye ndege wakielekea visiwa vya Madagasca na huko tunawekukaa kwa muda wa siku kadhaa ili kujipanga upya katika hili jambo lililo jitokeza”

“Ninaweza kuwasiliana nao?”

“Yaa unaweza”

Meja akafungua laptop iliyopo mezani kisha akaanza kuminya minya batani baada ya muda kidogo akanigeuzia. Sikuamini macho yangu baada ya kumuona Yemi akiwa katika hali ya usalama, tukajikuta tukishindwa kuzungumza kwa muda na machozi yakaanza kutumwagika taratibu taratibu.

“Yemi”

“Ndio mume wangu……upo hai kweli?”

“Ndio mke wangu nipo hai”

“Tumesaidiwa na watu ambao wala hatuwajui mume wangu vipi wewe?”

Yemi alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake.

“Hao ni rafiki zangu mke wangu”

“Kweli mume wangu?”

“Ndio na kwa sasa wanawapeleka Madagascar, tutaonana huko kwa masaa kadhaa”

“Ohoo asante Mungu kwa kutuepusha na kifo kwa maana nilisha kata tamaa kabisa”

“Ni kweli mume wangu”

“Muambie mtoto naye atangana nasi Madagascar, kazi ya kumkomboa imesha kamilika”

Meja alizungumza na kunifanya nizidi kujawa na furaha.

“Dany ni nani huyo anaye zungumza?”

“Ni rafiki yangu, anasema mtoto wetu yupo salama salmini”

“Kweli?”

“Ndio mke wangu”

“Ohooo asante Mungu naomba nimsalimie”

Yemi alizungumza kwa furaha, nikaigeuza Laptop sehemu alipo kaa meja.

“Habari yako shemeji yangu”

“Salama shemeji yangu, yaani sijui hata niseme nini, umebadilisha giza kuwa mwanga kwenye maisha yetu na mume wangu. Yaani ninakushukuru sana Meja”

“Ni jukumu langu kuwasaidia nyinyi kwa manaa mume onewa katika hili”

“Kweli shemiji yangu, yaani nina rudia tena na kusema Mungu akubariki wewe na watu wako”

“Amen tutaonana Madagascar”

“Asante”

Meja akanigeuzia laptop, tukatazamana na Yemi laiti ingekuwa tupo karibu basi tungekumbatiana kwa furaha sana.

“Natamani kukuona hata sasa hivi mume wangu”

“Usijali mke wangu tutaonana hapo”

“Nakupenda sana mume wangu kuliko kitu chochote kwenye maisha yangu”

“Ninakuopenda pia mke wangu”

Tukamaliza kuagana na Yemi na kukata mawasiliano haya kwa njia ya kuonana.

“Mapenzi yenu yananikumbusha mbali sana, kipindi nilipo kuwa kikazi nje ya Marekani, nilikuwa ninazungumza hivyo na marehemu mke wangu, ila ndio hivyo yalitokea yakutokea kama nilivyo kueleza na sikuwa na jinsi ya kufanya tena”

Meja alizungumza kwa sauti ya unyonge kiasi. Nikabaki nikimtazama usoni mwake kwa haraka haraka anaonekana ni mtu ambaye bado anaishi na upendo wa mke wake hadi leo akiwa katika uzee wake.

“Kwa nini umeamua kunisaidia?”

“Nilijua tu utaniuliza swali hilo mara baada ya kufika hapa”

“Ndio kwa maana maisha yangu nilisha yatoa kwa ajili ya kufa, maisha yangu nilisha yaweka mikononi mwa Mungu wangu kwani nilisha tambua kwamba siwezi kufanikiwa kutoka mikononi mwa watu walio nisaliti”

“Hilo ndio lilinifanya nikusaidie, sipendi usaliti kwenye maisha yangu na wala sipendi mtu msaliti kwa sababu usaliti ulinifanya maisha yangu niishi pasipo mwanamke ninaye mpenda, kisa kazi yangu ambayo kwa sasa nimesha iacha nimeamua kuachana na maswala ya jeshi”

“Umeacha kazi!!?”

“Ndio nimeacha kazi na nimeamua kumiliki jeshi dogo la vijana wangu ambao niliwafundisha mambo mengi na wana ujuzi mkubwa kuliko hata wanajeshi waliomo ndani ya nchi yangu na ninaimani kwamba umeweza kushuhudia kazi walio ifanya”

“Ndio nimeshuhudia, yaani kila kitu walicho kifanya hadi sasa hivi ninahisi ni ndoto ambayo dijui yaani imeishaje ishaje?”

“Hahahaaa sio ndoto rafiki yangu. Raisi wetu aliamua kukusaliti isitoshe akamchukua mwanamke ambaye unampenda kwenye maisha yako japo uliamua kufanya mabadiliko ya moyo wako ila Hawa ulimpenda si kweli?”

“Ndio nilimpenda ila kwa sasa siwezi kufanya hivyo kwa maana amenisaliti sasa sijajua ni kitu gani amepewa na raisi huyo?”

“Raisi amekuwa akiiendesha serikali ya Marekani kwa ubinafsi sana, na hapa ninavyo kuambia ni kwamba amemuacha mke wake kwa ajili ya Hawa”

“Hilo ninalitambua na Hawa ndio alimshauri raisi kuweza kumuacha mke wake haraka iwezekanavyo”

“Dany unatakiwa kufanya kitu katika hili, huwezi kuwaacha waishi kwa amani, namna hiyo ikiwa tayari amesha haribu mfumo wako mzima wa jeshi ambalo liliweza kufwata sheria yako pasipo kipingamizi cha ina yoyote”

“Kweli meja nitahakikisha ninaishangaza dunia katika hili”

“Katika hilo nina imani kwamba utanisaidia kwa asilimi mia moja kwa maana ninahitaji kuiongoza Marekani, ninahitaji Marekani iwe mpya iwe na nguvu, na isiongozwe na raisi anaye sikiliza mawazo ya mwanamke ambaye ni ninaweza kumfananisha na Malaya na amemucha mwanamke ambaye tunamtambua kikatiba”

“Unahitaji kuwa raisi?”

“Ndio”

 ITAENDELEA


0 comments:

Post a Comment

BLOG