Search This Blog

Wednesday, November 18, 2020

AIISSII U KILL ME LEGACY SEHEMU YA 1/10


AIISSII U KILL ME LEGACY

WRITER…………………………………………EDDAZARIA G.MSULWA
WEBSITE………………………………………… www.storyzaeddytz.com
CONTACT……………………………………….. 0657072588/0768516188
AGE……………..18+

SEHEMU YA 1 KATI YA 10

 


Taratibu nikanyanyuka kwenye sofa nililo kalia huku macho yangu yote yakiwa kitandani kwa wasichana wawili nilio toka nao Club usiku huu. Jinsi wanavyo nyonyana ndimi zao huku macho yakiwa yamewalegea wakanifanya nizidi kusisimka mwili wangu.

Nikapiga fumba la mwisho la pombe kali aina ya Bacrays, nikaiweka glasi juu ya meza hii ya kioo, kisha nikatingisha kichwa kidogo ili kujiweka sawa kwa maandalizi ya kuwashuhulikia wasichana hawa wawili. Kwa hatua za matamanio huku jogoo wangu akiwa amesimama kisawa sawa, nikaanza kuwasogelea wasichana hawa hadi kitandani.

“Unataka tukufanyie nini bosi?”

Msichana mmoja alizungumza kwa sauti nyororo huku akiendelea kunikodolea macho yake makubwa mithili ya gololi.

“Chohote mutakacho warembo”

Mmoja akaninyooshea mkono wake wa kulia, taratibu nikaupokea na akanivuta kitandani na kunilaza chali. Wakaanza kukinyonya kifua changu taratibu huku mikono yao ikipeana zamu ya kuingia katika boksa yangu iliyo nibana mwilini mwangu kisawa sawa.

“Waooooo!!”

Mmoja wao alizungumza kwa mshangao mara baada ya kumuona Jogoo wangu akiwa amesimama kisawa sawa na ana ujazo wa kutosha ambao kwa mwanamke yoyote ambaye anamuona ni lazima atatamani kupata japo ladha yake.

“Nyonya”

Nilimuambia msichana huyo huku nikiwa nimeishika shingo yake kwa mkono wangu wa kulia, taratibu akaushusha mdomo wake na kumuingiza jogoo wangu mdomoni mwake na kuanza kumnyonya. Mkono wangu wa kushoto ukawa na kazi ya kucheza na kitumbua cha mwenzake huyu anaye endelea kujitahidi kunyonya chuchu zangu ndogo za kifua changu hichi kilicho gawanyika kutokana na mazoezi ninayo yafanya kila siku.

“Ooohoooo….aaiiis…….”

Mwenzake akazidi kulalamika kwani kwa jinsi ninavyo jitahidi kucheza na kitumbua chake ni dhairi kwamba msisimko anao upata umemkolea. Nilipo ridhika na huduma ya kunyonywa na wasichana hawa, nikafungua droo yangu ndogo iliyopo pembeni ya kitanda changu na kutoa pakti moja ya kondom na kuivaa.

“Nani aanze”

Niliwauliza huku nikiwatazama wote. Hawakunijibu zaidi ya mmoja wao kunibong’olea. Taratibu nikaanzisha jaramba ambalo siku zote nikiwa na msichana mmoja hawezi kunikidhi mahitaji yangu na endapo atajitahidi kunihimili basi ni lazima apoteze fahamu. Kwa mpute mpute huu, wasichana hawa wakawa na kazi ya kubadilishana mikao tu, huku wakimwagikwa na jasho kwenye miili yao. Japo chumba changu kina A/C na feni la juu ila mtanange huu ni wa kukata na shoka.

“Unakoj*** saa ngapi?”

Msichana mmoja aliuliuliza huku akiwa anahema kana kwamba amekimbia mita elfu moja bila ya kupumzika.

“Kwani tataizo lako ni nini, si nina walipa”

Nilijibu huku nikiwa nimekishika kiuno cha mwenzake kisawa sawa.

“Mmmmm hata kama ila sijawahi kukutana na mwanaume kama wewe au unatumia madawa ya kuongeza nguvu?”

“Mbona una maswali ya kijinga hivyo. Unataka pesa au hutaki?”

“Nataka”

Msicha huyu alinijibu kwa unyonge sana huku akinitazama usoni mwangu.

“Na ukae kimya sasa. Na wewe bonyea vizuri”

Nilizungumza huku nikikishusha kiuno cha msichana huyu na kumfanya alalie tumbo lake kabisa. Nikaendelea na mtanange wangu hadi nilipo anza kujihisi haja ya kuwatoa waarabu weupe ndipo nilipo zidisha kasi hadi msichana huyu kilio cha raha kikabadilika na kikawa kilio cha machozi.

“Ooohoo Fuc**”

Nililalama kwa raha huku nikisikilizia jinsi utamu huu ninavyo upata. Nilipo hakikisha kwamba waarabu weupe wote wametoka, nikajitoa mgongoni mwa msichana huyu, nikashuka kitandani mwangu na kuingia chooni, huku nikishusha pumzi. Taratibu nikaichomoa kondom hii iliyo jaa waarabu wangu weupe, nikaidumbukiza kwenye choo changu cha kukaa na kuyafungulia maji yenye nguvu na yaka wasindikiza waarabu wangu hawa weupe na wakapotea kwenye upeo wa macho yangu. Nikameza fumba zito la mate huku nikijitazama kwenye kioo kilichopo bafuni humu, nikafungua mlango kidogo na kuchungulia chumbani.

“Heii njooni tuoge”

“Nyonga”

Msicha ambaye ndio wa mwisho kumaliza naye mchezo alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.

“Zimefanyaje?”

“Zinauma kaka yangu nashindwa hata kusimama”

“Na wewe”

“Ninakuja”

Msichana huyo akamsaidia rafiki yake kushuka kitandani, kwa mwendo wa taratibu wakafika bafuni humu, kwa ishara ya mkono nikawaonyesha waweze kuingia kwenye sinki la maji na wataogea humo. Nikarudu chumbani na kuyatoa mashuka yote kitandani na nikayaingiza kwenye ndoo maalumu ya kuwekea nguo chafu. Nikarudi bafuni na kuwakuta wasichana hawa wakiendelea kuogeshana taratibu.

“Tulikubaliana kiasi gani?”

“Naira…….”

“Sina pesa ya Nigeria kwenye wallet yangu na wala sitembei na pesa hiyo semeni ni dola ngapi?”

Wasichana hawa wakatazamana huku wakitabasamu, kweli mbele ya pesa hata mgonjwa ana weza akapotea upako wa uponyaji.

“Dola efu moja”

“Kwa kila mmoja au?”

Wakaendelea kunikodolea macho yao na kukosa jibu la kunipatia, kwani kiasi nilicho watajia

“Kila mmoja nitampa dola elfu moja sawa”

“Ohoo asante wee kaka. Hivi unaitwa nani ili siku nyingine ukija pale kwenye club yetu tuwe tunakupa huduma kama hii?”

Nikatabasamu kidog huku nikirudu chumbani, nikachukua suruali yangu niliyo ivua na kuiweka juu ya sofa, nikachomoa wallet yangu na kurudi nayo bafuni.

“Sina utaratibu wa kurudia wasichana, na sinto hitaji mukatangaze juu ya kufanya mapenzi na mimi na endapo mkifanya hivyo na nikafahamu, shingo zenu zitakuwa ni halali yangu”

Nilizungumza kwa kujiamini huku nikichomoa noti ishiri za dola mia mia, nikamkabidhi kila mmoja kiasi chake hicho huku wakiwa na mshaka kutokana na kile kitu nilicho kizungumza.

“Mumenielewa?”

“Eheee”

Walitingisha kichwa wakiwa wamejawa na wasiwasi mwingi sana.

“Na mutalala hadi asubuhi, sawa”

“Sawa bosi”

Tukamalia kuoga kwa pamoja na kurudi chumbani, nikachomo moja ya shuka kwenye kabati langua la nguo na kuwakabidhi watandike kitanda hichi.

“Kaka”

“Naam”

“Unaitwa nani?”

“Aisee nimewaambia swala la jina langu haliwahusu au kuna jengine munalo hitaji?”

Nilizungumza kwa ukali kidogo huku nikiwakazi amacho wasichana hawa.

“Ndio mimi kuna kitu ninacho kihitaji?”

“Nini?”

“Nimetokea kukupenda kaka yangu”

“Hahaaaa, dada hii ni Nigeria, ulisha wahi kuona wapi malaya akampenda malaya mwenzake. Hicho kitu hakipo na wala musijisumbue kunipenda wala kuniwazia, na wala musiweka mategemeo ya kuja kuniona tena kwenye maisha yenu”

Maneno yangu yakazidi kuwapa utata wasichana hawa. Nikapanda kitandani, mmoja akalala upande wa kulia na mwengine akalala upande wa kushoto kwangu huku wote wakiwa wamevilaza vichwa vyao kifuani mwangu. Haukupita muda mrefu usingi mzito ukanipitia na nikalala fofofo.

***

“Randy ni upumbavu gani unaufanya ndani ya nyumba yangu eheeeeee?”

Sauti kali ya mama ikanistua kutoka usingizini, nikatazama pembeni yangu na kuwakuta wasichana hawa wawili nilio lala nao toka jana usiku wakijitahidi kuamka kitandani. Macho yakanitoka huku nikimtazama mama yangu akiwa amesimama kwa ukali kwa haraka nikachukua mto na kujifunika sehemu zangu za siri, kwani ujio wa mama sikuutegemea kwa asubuhi ya siku ya leo.

“Shikamoo ma…..”

“Nyinyi machangudoa, nikifumba macho na kufumbua sihitaji kuwaona ndnai ya nyumba yangu, tokeniiiii”

Mama alizidi kufoka na kuwafanya wasichana hawa kushuka kitandani na kila mmoja akaanza kutafuta ni wapi ambapo anaweza kuziona nguo zake.

“Pumbavu, walinzi njooni munitolee hii mizoga”

Wakaingia walinzi wawili wa mama ambao siku zote huwa siwapendi kwa maana wao ndio huwa wanawasimamia hadi walinzi wangu na kila ninalo lifanya basi huwa linamfikia mama kwa haraka sana hata akiwa yupo nje ya nchi hii ya Nigeria.

“Waondoeni na munajua nini munapaswa kufanya”

“Sawa mkuu”

Wasichana hawa wakabebwa juu juu na kutolewa ndani humu huku wakiwa uchi kabisa.

“Mam…………..”

“Funga bakuli lako, pumbavu wewe. Unahisi kutembea na hawa wasichana ni jambo lenye usalama, eheee?”

“Ila mama si?”

Mama akaokota glasi iliyopo mezani akanirushia kwa nguvu, kwa bahati nzuri tukio hilo niliweza kuliona na nikafanikiwa kuikwepa glasi hiyo na ikabamiza ukutani na kubanjika banjika.

“Siku nikikusikia ukiongea mbele yangu huku nikiwa nimekasirika nitakuvunja hicho kichwa chako. Oga haraka iwezekanavyo, ninahitaji tuelekee ofisi sasa hivi sawa”

“Sawa mama”

Niliitikia kwa unyonge sana kwa maana siku zote mama yangu amekuwa ni mtu mwenye kukasirika na mara kwa mara kadhaa huwa anafanya maamuzi ya ajabu ambayo mengi hupelekea kuwaangamiza hata wafanya biashara wezake pale tu anapo tiwa hasara au kukosewa kidogo. Mama akaanza kutembea kuelekea mlangoni, akaubamiza mlango wa mwangu kwa nguvu na kuniacha kitandani hapa nikitafuta pozi la kusimama.

“Fuc***”

Nilizungumza kwa sauti ya chini huku nikishuka kitandani, nikaingia bafuni na kuoga. Nikarudi chumbani mwangu, nikafungua kabati ninalo hifadhia suti zangu. Nikalitazama kwa muda kidogo mpangilio wa suti hizi na nikachagua suti moja nyeusi, nikaivaa na shati lake jeupe pamoja na viatu vyeusi. Nilipo hakisha nipo vizuri, nikatoka chumbani humu huku nikiwa nimeshika tai yangu nyeusi mkononi. Nikashuka kutoka gorofa la pili hadi katika seble iliyopo katika eneo la chini. Nikamkuta mama akiwa amekaa sebleni akitoa maelekezo kwa meneja wake mzee Uchuku.

Mama akanitazama kwa jicho kali lililo jaa hasira, kabla hata sijafungua kinywa changu, akaninyooshea kidole kwamba nielekee kwenye meza ya chuakula. Taratibu nikaelekea kwenye meza ya chukula, wadada wawili wa kazi wa hapa nyumbani wakaanza kunihudumia.

“Inatosha”

Nilizungumza huku nikimzuia dada huyu kuniwekea kiwango kikubwa cha maji ya moto kwenye kikombe changu. Mama akafika kwenye meza hii na kukaa kwenye kiti chake ambacho hakikaliwi na mtu yoyote hata kama akiwa amesafiri.

“Ondokeni”

Mama aliwaambia wafanyakazi hawa wa ndani, wakainamisha vichwa vyao chini kidogo kama ishara ya heshima kisha wakaondoka katika eneo hili na kutuacha mimi na mama.

“Swala la kutembea na malaya nilikuambiaje?”

“Ehhe……?”

“Hujanisikia au?”

Mama kidogo akapandisha sauti yake.

“Naomba unisamehe?”

“Hivi unahisi hizi pesa zangu ninazitafuta kwa ajili yako eheee?”

Kauli ya mama ikabaki ikinishangaza kwa maana katika maisha yangu ninafahamu kwamba mimi ndio mtoto wake wa pekee na hana mtoto mwengine zaidi yangu.

“Pesa ninayo itafuta ni kwa ajili yangu mimi peke yangu. Sasa na wewe ukae utafute pesa zako. Mtoto una miaka ishirini na mbili ila umeendekeza umalaya, hivi utafuti mwanamke mmoja ambaye atakukithi mahitaji yako?”

“Mama……”

“Sitaki kusikia upuuzi na kuanzia hivi ninavyo zungumza, kila kitu utakacho kifanya ni lazima unipe taarifa. Umenisikia Randy”

“Ndio mama?”

“Tena nipe funguo za Benzi yako”

Mama alizungumza huku akininyooshea mkono, taratibu huku nikiwa nimejawa na unyonge mwingi sana, nikaingiza mkono wangu mfukoni na kutoa funguo ya gari langu ninalo lipenda sana na nikamkabidhi.

“Sitaki nione unachukua gari ya aina yoyote humu ndani na akaunti zako zote za benki nimeagiza meneja azifunge zote”

“Khaaa mama huo ni uonev……”

Nikajikuta andazi likinipiga usoni mwangu jambo lililo zidi kunikasirisha.

“Nimekuambia nikizungumza, sitaki kupingwa umenielewa mjinga wewe?”

“Mama katika hilo hapa, hata kama ni za kwako, nitazungumza. Ni haki yangu kuzungumza na mama yangu kwa kile ambacho ninahisi kwangu sio sahihi”

“Randy funga bakuli lako nitakuvunja sehemu”

“Nivunje tu mama, ninafaida gani ya kuwa mtoto wa mwanamke namba moja tajiri Afrika eheeee?”

Nilizungumza huku machozi yakinimwagika usoni mwangu.

“Faida, faidi unaijua wewe eheee?”

Mama alizungumza huku akisimama na kuanza kunifwata taratibu katika sehemu nilipo kaa, taratibu nikasimama na kuwafanya walinzi wote wanne wa mama kunitazama kwa umakini.

“Mtoto wa kiume unajiliza liza kisa mali zangua mbazo nilizipigania kufa na kupona kutoka kwa wajinga walio kuwa wamejirithisha, eheee?”

Mama alizungumza huku akisimama mbele yangu. Mama yangu kwa sura ni mwanamke mzuri sana, ila rohoni mwake ni mwanamke ambaye hadi sasa hivi nimekosa jina halisi la kuweza kumpa. Akanipiga makofi mfululizo kwenye shavu la upande wangu wa kulia, jambo lililo nifanya niyafumbe macho yangu huku nikiendelea kusikilizia jinsi anavyo nitandika makofi yake kwa uchungu.

“Unajua faida mjinga wewe, eheee”

“Mama utanipiga hadi uniue, ila leo nitahitaji kumfahamu baba yangu. Ninahitaji kumjua baba yangu halisi hata kama amekufa nionyeshe kaburi lake na si kuendelea kuishi maisha ya kunyanyasika kwa mama yangu, au mimi sio mwanao eheeee?”

Nilizungumza kwa ukali huku machozi yakindelea kunitoka machoni mwangu. Mama akasitisha zoezi la kunipiga vibao, nikaanza kuyasikia meneno yake jinsi yanavyo sagana mdomoni mwake kwa hasira aliyo nayo na hata kuzungumza anashindwa.

“Niambie mimi sio mwanao mama eheeee?”

Mama akaka kama dakika mbili hivi akinitazama, kisha akatabasamu kwa hasira kidogo.

“Unataka kumjua baba yako si ndio?”

“Ndio ni vyema ukaniambia baba yangu, kwenye maisha yangu yote nimekaa bila baba, umekuwa ni mtu wa kunidanganya danganya kila siku. Ni bora hata nikamfwata baba yangu popote alipo duniani, kuliko kuendelea kuwa hivi mama”

Niliendelea kuzunumza kwa kulalama, mama akarudi hatua chache nyuma, akachomoa bastola yake kiunoni na kuninyooshea usoni mwangu.

“Huyu ndio baba yako, huyu ndio aliye nitia mimba yako. Sasa msalimie baba yako”

Mlio wa risasi ukanifanya nistuke sana na mwili wangu mzima ukaanza kunitetemeka huku nikimtazama mama akishusha mkono wake ulio shika bastola chini taratibu na risasi aliyoipiga pembeni yangu imevunja kioo kilicho nyuma yangu.

“Siku ukiwa jasiri kama baba yako, nitakueleza baba yako ni nani na alikuwa ni nani, ila ukiendelea kuendekeza kumtomb** huto mjua baba yako hadi unakufa.”

Mama baada ya kumaliza kuzungumza akaanza kuondoka na kuniacha nikiwa na maswali mengi sana huku hamu ya kuendelea kumfahamu baba yangu ikiwa ni kubwa sana kupita siku zote za maisha yangu.



Taratibu nikanza kumfwata mama huku nikimuita, mama hakugeuka hadi alipo fika kwenye mlango wa gari lake.

“Nini?”

“Mama nahitaji kuzungumza na wewe?”

“Ingia kwenye gari”

Mama alizungumza kisha akaingai kwenye gari na mlinzi akafunga mlango, nikazunguka upande wa pili wa gari na kuingia. Safari ikaanza ya kutoka katika jumba letu hili la kifahari na kuelekea katika ofisi za kampuni ya mama inayo shuhulika na maswala mengi sana ndani na nje ya nchi hii ya Nigeria.

“Mama”

“Mmmm”

“Naomba uweze kuniambia baba yangu ni nani?”

“Kwa muda huu sina muda wa kulizunngumzia hilo swala, kuna mambo mengi sana ambayo tunatakiwa kuweza kuyafanya leo”

Sikuwa na la kuzungumza zaidi ya kukubaliana na mama kwa kile alicho kizungumza. Tukafika ofisini na moja kwa moja tukaelekea hadi ofisini kwa mama, kilicho nishangaza ni kuwakuta baadhi ya viongozi wa kiserikali wakiwa wanamsubiria mama. Mama akasalimiana nao kwa heshima zote, kisha nami nikawasalimia.

“Tunaweza kwenda kwenye ukumbi wa mikutano”

Mama alizungumza huku akiwaonyesha mlango wa kutoka humu ofisini. Viongozi hawa wanne huku mmoja akiwa ni mkuu wa majeshi wakanyanyuka kwenye viti vyao na kutoka ofisi humu kwa mama.

“Mama”

“Nini?”

“Kuna nini kinacho endelea?”

Nilimuuliza mama kwa sauti ya chini.

“Sio kila kitu unatakiwa kukifahamu. Nenda ofisini kwako na ukaendelee na shuhuli zako sawa”

Mama baada ya kumaliza kufanya hivyo, akatoka ofisini humu na kuniacha peke yangu. Nikshusha pumzi taratibu kisha nikatoka ofisini kwake na kuelekea katika ofisi yangu, kila ninapo pita wasichana na wafanyakazi wa kiume hawakusita kunisalimia.

“Bosi bosi”

Sekretari wangu aliniita.

“Ndio”

“Kuna maombi yameletwa hapa kuna tv moja inahitaji tuweze kupelekea matangazo yetu katika kitua chao cha tv”

“Tukaongelee ofisini”

Nilizungumza kwa ufupi huku nikifungua mlango wa chumba changu cha ofisi, nikaitazama ofisi hii, ila kusema kweli sina furaha kabisa katika siku ya leo japo nimemfanyia makosa mama yangu, ila si kwa kuwa mbabe kiasi hichi. Kila kitu anacho kizungumza sekretari wangu wala sikuweza kukisikia, japo anazungumza kwa sauti ya juu kidogo, ila mawazo yangu yapo mbali sana.

“Bosi”

Sekrtari wangu aliniita huku akiwa amenishika mkono.

“Ndio ndio”

“Ninakuongelea ila ninakuonaa haupo hapa”

“Ooho samahani Diana, ehee hembu niambie maombi yao yanataka nini?”

“Wanahitaji tukaweke matangazo kwenye baadhi ya vipindi vyao, kwa mwenzi mzima watatufanyia bure kisha baada ya hapo basi watatufanyia kwa pesa”

“Ni kituo gani?”

“EChanel”

Nikafunga macho yangu kwa muda, kisha nikashusha pumzi na kuichukua barua hii ya maombi, nikaipitai kw amuda kidogo kisha nikamrudishia Diana.

“Hakikisha kwamba linaenda hili tangazo la ofa za kupiga simu kwenda mitandao mingine kwa kiwango kidogo”

“Sawa bosi”

Diana akaanza kutembea hadi mlangoni, huku nikiyasindikiza makalio yake kwa macho jinsi yanavyo tingishika kutoka kulia kwenda kushoto, kushoto kwenda kulia.

“Hei Diana”

“Ndio Bosi”

“Aha…..basi”

“Kuna tatizo lolote bosi?”

“Hakuna, nikikuhitaji nitakupigia simu”

“Sawa mkuu”

Diana akafungua mlango na kutoka. Kitengo ninacho fanya kazi kama meneja masoko katika mtanado wetu wa simu uitwao Dellcal, ninakiendesha vizuri jambo linalo fanya kampuni hii kuzidi kupanda chati, na kusambaa katika nchi za jirani ya Nigeria kama Chad, Cameroon na Niger. Toka nianze kusimamia kitengo hichi ndani ya mwaka mmoja tu nilio fanya kazi, nimeweza kufanya kampuni kuingiza zaidi ya dola za kimarekani bilioni kumi, ikiwa nimevuka malengo ya dola bilioni tano kwa mwaka mmoja. Japo nina madhaifu yangu ya kupenda sana wasichana ila katika swala zima la kibiashara nipo vizuri sana.

Nikaanza kupitia ofa ambazo tumezipokea kutoka kwenye mashirika makubwa, moja baada ya nyingine. Ila kila ninavyo jaribu kufanya kazi zangu, ninajikuta sentensi ya mama kijirudia kichwani mwangu. Nikatoa simu yangu mfukoni na kumpigia Alex rafiki yangu ambaye muda mwingi ndio mshauri wangu wa mambo mengi binafsi.

“Njoo ndani”

Nilizungumza kwa ufupi kisha nikakata simu. Hazikupita hata dakika tano, Alex akaingia ofisini kwangu, tukasalimiana kama kawaida.

“Ehee kaka hembu niambie wale watoto jana usiku uliondoka nao?”

“Yaaa, yaani ni bora hata ningelala nao huko hotelini. Bi mkubwa si alirudi bila ya mimi kujua na akanikuta nao nimelala nao”

“Weeee”

“Yaani, sijui watoto wa watu watakuwa wapi muda huu, kama unavyo muelewa mama si mtu wa mchezo mchezo”

“Mmmm ndio maana nilikutana naye akielekea katika ukumbi wa mikutano, nikamsalimia, ila hakutikia”

“Yaa amenishikia hadi bastola”

“Mmmm!!!”

“Oho mama kachafukwa, sijui ni kina nani wamemuuzi na akili yangu yote nilijua anarudi kesho, ila sikui alirudi muda gani, na sijui ilikuwaje”

“Pole sana mshikaji wangu, ehee niambie”

“Nimekuita hapa kuna jambo la baba yangu linanisumbua sana akili. Nikimuuliza mama anaendelea kuwa mkali kama ilivyo kuwa siku zote, ila leo ameniambia ponti ambazo ninahitaji kuzitumia kuanza kuupata ukweli wa nani ni baba yangu”

“Pointi gani?”

“Amesema niweze kuwa jasiri kama baba yangu na ataniambia nani ni baba yangu”

“Uwe jasiri kama baba yako na atanieleza nani ni baba yako?”

“Yaaa”

“Mmmm hilo ni fumbo rafiki yangu”

“Ndio maana yake, ndio maana nimekuita hapa ili uweze kunisaidia kulifumbua fumbo hili”

“Sasa kwenye ishu ya ujasiri hapo ni ipi, kwa maana kama ni akili nzuri mbona unayo tu na kama ni mazoezi mbona unafanya kama kawaida”

“Ni kweli ndugu yangu ila inabidi nifanye jambo”

“Jambo gani?”

“Niache kazi”

“Samahani umesema”

“Niache kazi, nijiunge na jeshi kwa maana ndio kitu ambacho nilikuwa ninakipenda toka udogo. Nina miaka ishirini na mbili sasa hivi, elimu ninayo, najua nikisota mwaka wangu mmoja jeshi, nikiingia kazini nina pata cheo kizuri tu naamini kuanzia hapo nitauwa jasiri. Nahisi hivyo ndivyo nilivyo muelewa mama yangu”

“Sawa Randy, ila kumbuka kampuni inakutegemea na mbona muna kila kitu rafiki yangu?”

“Nyinyi ndio munaona nina kila kitu, ila leo asubuhi mama amenipokonya, gari, akaunti zote za benki zimefungiwa, na amenieleza kwamba hizi mali zote sio zangu, sasa hapo bila ya kujiongeza siwezi kufanikiwa na isitoshe nikisema kwamba nikaanzishe kampuni yangu. Sinto fanikiwa kwa maana nitakuwa ninatangaza uadui na mama, na nikitangaza uadui huo basi nitafilisiwa na nitarudi kwenye mikono yake”

“Mmmmm rafiki yangu hilo ni wazo zuri, silikatai kabisa, ila mbona unaweza kuanzisha kampuni yako hata katika nchi za Mashariki ya Afrika ambazo sio rahisi wewe kugundulika?”

“Humjui mama yangu, nchi zote Afrika ana makampuni, wapi ninakwenda kuanzisha kampuni ambayo yeye kama yeye hato ijua?”

“Duuu hapo kuna mtihani”

“Yaa, kitu ambacho nilicho kiona hapo, endapo nitaingia jeshi, basi ninaweza kuwa muajiriwa wa serikali na nitakuwa nikifanya kazi chini ya serikali na maisha yatasonga mbele au unasemaje?”

“Kweli ni wazo zuri, ila jeshini utaweza mwanangu, na ujue kuna hawa Boko haramu, picha haziendi kabisa na jeshi la nchi, usije ukawa miongoni mwa watu ambao watatolewa sadaka kwenda kupambana nao?”

“Nikifikiria hayo sinto fanya lolote, acha niaende kwanza inakavyo kuwa basi hivyo hivyo, kwani kufa kitu gani rafiki yangu”

“Mmmm”

“Ndio, nashukuru kwa ushauri nenda kaendelee na kazi zako”

“Vipi leo mitoko?”

“Mwanangu hunionei huruma, yaani sina gari, sina chochote. Nilicho achiwa hapa ni hizi nguo zangu na simu hii”

“Hahaa haya poa kaka”

“Ila vipi kitengo chako, kinakwenda?”

“Kinasogea rafiki yangu”

“Okay badae”

Alex akatoka ofisini humu, nikaka kama dakika kumi hivi kisha nikasimama kwenye kiti changu na mimi nikatoka.

“Diana raisi wa kampuni amemaliza vikao na wale wageni?

“Sijafahmu bosi”

“Unaweza kuniazima gari lako?”

“Gari langu!!!!!?”

Diana aliniuliza huku akiwa amejawa na mshangao mkubwa sana kwani hakuna siku hata moja niliwahi kumuomba gari lake.

“Ndio”

“Naomba uniazime”

Diana akafungua pochi yake na kunipa funguo ya gari langu. Nikamshukuru na nikaanza kutembea kuelekea katika lifti huku nikiwa makini sana, kwani walinzi wangu leo hii sifahamu wapo wapi. Nikaisubiria lifti hii inayo pandisha kutoka chini kuja juu ifunguke. Lifti ikafunguka nikajikuta nikiishiwa nguvu mara baada ya kukutana na walinzi wangu ndani ya lifti hii.

“Kuna sehemu unaelekea mkuu?”

“Ninakwenda kupunga hewa nje”

“Sawa ingia twende”

Nikashusha pumzi huku nikiwatazama usoni mwao, nikaingia ndani ya lifti na taratibu tukaanza kushuka chini.

“Mumekuja na usafiri wenu?”

“Ndio mkuu”

“Sasa sikilizeni, kuna sehemu muhimu sana ninahitaji niweze kwenda hivyo ninawaomba musiongozane nami?”

“Bila ya kukuvunjia heshima mkuu hilo swala haliwezekani.”

“Ninaweza kujilinda mimi mwenyewe”

“Hata kama ila hutuwezi kukuacha na ukitegemea sasa hivi ni muda wa kazi bado”

Tukafika chini kabisa, lifti ikafunguka, tukatazamaa na watu ambao wanasubiria kuingia katika lifti hii.

“Turudini juu”

Nilizungumza kwa ufupi huku nikigairi kwenda kule nilipo kusudia kwani ni sehemu ambayo sihitaji mtu yoyote weze kufahamu kwamba ninakwenda kwenye maeneo hayo. Tukarudi gorofa ya ishirini, zilipo ofisi kuu za kupuni hii ya mama. Nikiwa njiani kuelekea kwenuye ofisi zangu, kwa bahati nzuri nikakutana na mkuu wa majeshi, nikamsimamisha na nikamuomba niweze kuzungumza naye ofisini kwangu. Hakusita kunikubalia na tukaingia ofisini kwangu. Nikamueleza haja yangu ya kujiunga na jeshi la serikali, kwa mara ya kwanza akashangaa sana, ila nikaendelea kumshawishi hadi ombi lamwisho akaniomba niweze kuzungumza na mama yangu na endapo mama yangu atakubaliana basi nitajiunga na jeshi. Nikaagana naye, nikamsindikiza hadi kwenye lifti kisha nikaelekea ofisini kwa mama.

“Mbona leo hutulii ofisini kwako, ninakuona unakatiza katiza tu?”

“Ninahitaji kuzungumza nawe”

“Kmaa ni maswala ya nyumbani yakazungumziwe nyumbani sawa?”

“Sio swala la nyumbani, ila ni swala la hapa kazini”

“Zungumza?”

“Ninahitaji kuacha kazi, sihitaji kuwa mfanyakazi wa hii kampuni?”

Mama taratibu akanigeukia na kuacha kusoma kile alicho kuwa anakisoma kwenye computure yake iliyopo juu ya meza.

“Unasema?”

“Ninahitaji kuacha kazi, sitaki kuwa mfanyakazi wa hii kampuni tena”

“Hivi unajua wewe ni mpumbavu, mjinga mzembee eheee?”

Mama alianza kufoka.

“Hivi mama mbona hupendi kunipa nafasi ya kujielezea una kazi ya kukaa na kunitukana eheee?”

“Hilo ndio lililo kutoa ofisini kwako na kuja kuniambia ujinga huo?”

“Sio ujinga, kwa maana ninafanyaje kazi kwenye sehemu ambayo sina faida nayo. Sehemu ambayo ninajua kabisa kwamba mali si zangu, eheee. Niache nikatafute mali zangu, niache nikaanze maisha ya kuishi uswahilini na masikini wengine, kuliko kuishi kwenye mgorofa mkubwa ambao hauna faida yoyote kwenye maisha yangu. Nisifanye jambo ninalo lipenda, kwako ni baya”

Nilizungumza kwa msisitizo huku nikimtazama mama usoni mwangu.

“Mimi ni mwanaume, ninatakiwa siku moja niwe na familia yangu, niwe na watoto wangu na niwe na mali zangu, na kama ulivyo niambia asubuhi, ninatakiwa kuwa jasiri kama baba yangu, ili niambie, ila naona sasa nitakua jasiri zaidi ya baba yangu. Ninahitaji kujiunga na jeshi, nitakuwa tayari kufa au kupona ila najua nikitoka hapo nitapokea mshahara wa serikali na si mshara wa mikono yako”

Mama akaka kimya huku akinitazama kwa kunikazia macho.

“Na swala la kumtafuta baba yangu wala lisikupe tabu sana moyoni mwako, nitamtafuta mimi mwenyewe baba yangu, na wala sinto hitaji unisaidie kumtafuta na kuanzia hivi sasa hao panya wako ulio niwekea wanifwate fwate nyuma kama kumbikumbi sitaki kuwaona sawa mama”

“Umemaliza?”

“Ndio”

“Weka simu yangu mezani, na vua kila kitu ambacho ulinunmua kwa pesa yangu, kisha utoke humu ofisini kwangu”

Nikamtazama mama kwa muda kidogo kisha nikaanza kuvua koti hilo la suti, nikaitoa simu yangu mfukoni na kuiweka juu ya meza, nikavua shati, saa kisha nikafwata na suruali na vyote nikaviweka juu ya meza yake.

“Sijajua ni kwa nini una nichukia, sijajua ni kwa nini umekuwa ni mama wa tofauti sana kwenye maisha yangu. Wezangu wanajivunia kuwa na mama wenye upendo, wenye kujali, ila wewe umekuwa ni mama katili kwangu toka mtoto na nilikuuliza au mimi sio mwanao ila hujanipa jibu ila umenidhiirishia kwamba mimi sio mwanao, mimi ni mtu baki ndio maana umenivua hadi nguo ambaozo nimenunua na pesa yako. Nashukuru kwa hilo mama, acha nikatafute maisha yangu kwa maana mimi ni mwanaume nitapambana”

Nilizungumza huku machozi yakinimwagika usoni mwangu. Nikaanza kutembea kuelekea mlangoni.

“Unaenda wapi na hiyo boksa. Vua na utoke hivyo hivyo ukaenze maisha wewe si jeuri, mimi ni jeuri zaidi yako pumbavu wewee”

Mama alizungumza kwa hasira huku machozi yakimlenga lenga usoni mwake. Nikashusha pumzi kisha nikaivua boksa na kumrushia mezani mwake kisha nikatoka ofisini kwake nikiwa uchi kama nilivyo zaliwa jambo lililo washangaza watu waliopo ofisini humu kwa mama.



Mlinzi mmoja wa mama kwa haraka akavua koti lake na kulizungusha kiunoni mwanga ili kuepuka aibu ambayo ninaendelea kuipata. Nikalishika koti hili vizuri na kuzidi kusonga mbele huku kila ninapo pita wafanyakazi wananishanga.

“Randy, Randy ni nini kilicho tokea?”

Alex aliniuliza huku akwia amejawa na mshangao mkubwa sana. Sikumjibu kitu cha aina yoyote zaidi ya kuendelea kusonga mbele huku hasira ikiendelea kuchemka kifuani mwangu. Tukaingia wote kwenye lifti na taratibu ikaanza kushuka kuelekea chini.

“Randy rafiki yangu nini kimekutatiza?”

“Sipo sawa ninakuomba uniache”

“Hapana Randy, kumbuka mimi ni rafiki yako mshikaji wangu”

“Nimekuambia niache, rudi ukaendeleee na kazi sawa”

Nilifoka hadi Alex akatetemeka kidogo, kwa maana nimekuwa ni mtu mwenye hasira sana. Lifti ikafunguka, nikatoka kwenye lifti hii na kuanza kutembea kuelekea nje, nikakutana na Diana akiwa anashuka kwenye gari lake na sifahamu alikwenda wapi mara baada ya kumrudishia fungua.

“Bosi ni nini kimekupata!!?”

Diana aliniuliza huku akiwa amejawa na mshangao mkubwa sana

“Naomba unisaidie kiasi chochote nikanunue nguo”

Diana akafungua kipochi chake kidogo na kunikabidhi noti moja ya dola mia.

“Kwa heri ya kuonana, kuanzia hivi sasa mimi sio bosi wako wala mfanyakazi wa hii ofisi?”

“Nini, hapana unanitania kwa kweli Randy”

“Ndio hivyo, ninakutakia uwajibikaji mwema katika kazi zako”

Baada ya kumaliza kuzungumza hivyo nikaendelea kutembea, Diana akaanza kunifwata kwa nyuma huku akiniita, ila sikusimama. Nikafika getini, wote nao wakashangaa kuniona nikiwa hivi.

“Mkuu una tatizo?”

“Fungueni geti?”

“Ila mbo……”

“Munataka kazi hamtaki kazi eheeee?”

Nilizungumza kwa kufoka, kwa jinsi nilivyo kuwa mcheshi kwa wafanyakazi hawa, kitendo cha kuwafokea kwa kweli kila mmoja kikamstua sana na kujua kwamba leo nimekasirika.

“Bosi naomba uingie ndani ya gari?”

Diana alizungumza huku akinitazama akiwa ndani ya gari lake.

“Tafadhali Randy naomba uingie ndani ya gari”

“Sijakuomba unisaidie”

“Nalijua hilo mkuu, ila ninakuomba tafadhali, ingia ndani ya gari”

Nikajifikiria kwa muda, kisha nikafungua mlango wa gari na kuingia ndani. Mlinzi mmoja akafungua geti hili la meme na taratibu tukaanza kutoka ndani humu,

“Randy hembu naomba uniambie ni nini kilicho tokea, natambua una hasira, ila kama nilivyo mtu wako wa karibu ninakuomba uniambie bosi wangu?”

“Mimi sio bosi wako, wewe endelea kuniita Randy”

“Sawa nimekuelewa, ninakuomba uniambie sasa”

Nikashusha pumzi taratibu, nikaanza kumuadithia matatizo na visa ambavyo ananifanyia mama yangu. Kila nilicho muambia Diana anashangaa sana, kwani matukio mengine ni ya aibu sana kwa mama kumfanyia mwanaye hususani wa kiume.

“Kwa msaada huu, unaweza kufukuzwa kazi?”

“Randy kama wewe haupo ofisini na mimi nipo tayari kuacha kazi muda wowote, nimekuzoea, kwa mwaka mmoja tu ambao umekaa katika ile kampuni umenifanya nifanikiwe na kupata madili mengi sana ya makampuni yakihitaji kufanya nami kazi, ila nilikuwa sihitaji kutoka kutokana mimi na wewe kete zetu zinaendana bosi wangu””

“Usiache, nisije nikaonekana nimekushawishi na ukatoa siri na mipango tuliyo kuwa tunaifanya kufanikisha hii kampuni kusonga mbele, najua mwisho wake hauto kuwa mzuri kwako”

“Una maana gani?”

“Tutazungumza tukiwa free”

“Sawa, kwa sasa unaelekea wapi?”

“Sina sehemu ya kwenda, hii dola mia uliyo nipatia nitanunua nguo na ndio nitakayo anzia nayo maisha”

“Hapana Randy, ngoja nikupeleke kwangu, nikakuache kisha nirudi kazini. Jioni nikirudi tutazungumza vizuri”

“Shemeji akinikuta itakuwaje?”

“Haahaa, Randy yule mjinga nimesha achana naye?”

“Weee?”

“Haki ya Mungu, nachukia wanaume wanajeshi, wanahisi amri wanazo amrishwa huko jeshini basi wanaweza kuamrisha hadi mioyo ya watu, wakati sivyo, nilazima mwanamke abembelezwe na ajaliwe kwa kila jambo, na si kuleta ubabe, huwa tunawachoka mapema sana”

“Mmmmm”

“Mbona unaguna sasa?”

“Hamna kitu”

“Mmmm una uhakika?”

“Ndio”

Tukafika nyumbani kwa Diana alipo panga nyumba nzima na anaishi yeye, kijana wa kike anaye msaidia katika kusafisha safisha nyumba na kumfungulia geti. Nikashusha huku nikiwa nimelifunga koti la mlinzi huyu kiunoni, msichana huyu wa kazia aktusalimia huku akinishangaa.

“Ila Randy unavituko sana”

“Kwa nini?”

“Uliwezaje kutoka ofisi kwa mama yako ukiwa uchi kabisa?”

“Maamuzi Diana, na moyo pia ukichoka kama mtoto wa kiume, unaona ni bora kujitoa sadaka kuliko kuishi maisha ya kusimwangwa kana kwamba umezaliwa kwa bahati mbaya hapa duniani”

Tulizungumza huku tukieleeka kwenye kordo ambapo kuna milango mitatu ya vyumba vitatu tofauti.

“Sasa chumba hichi sijui mazingira yake utayapenda, kitanda chake ni kidogo ni nne kwa sita na mara nyingi hakitumiki”

Diana alizungumza huku akifungua mlango wa chumba hichi, tukakitazama vizuri. Ila kutoka nimesha amua kuishi maisha ya namna yoyote, nikakubali kukaa katika chumba hichi huku nikisubira kufanya kile ninacho kihitaji kukifanya kwa wakati huu.

“Kweli utaweza kulala humu Randy, au nimihamishe dada aje kulala huku?”

“Hapana, wewe kuwa na amani nitalala hapa, ila ningeomba msaada wa kupata japo hata buka ili niweze kuwa na amani, hivi unajua ndani ya hili koti sina kitu chochote?”

“Hahaa, ngoja nikakutafutie japo track yangu ya mazoezi naweza kukutosha”

“Mmmm si itanibwebwea”

“Na nini tena?”

“Na hiyo shepe mmm”

“Hahaa kwenda zako”

“Shem anafaidi”

“Jamani Randy mbona una vituko wewe”

Diana alizungumza kwa sauti laini kidogo huku akielekea chumbani kwake na mimi macho yangu yoye yakiwa katika makalio yake yanayo endelea kuniwewesa. Nikatazama sebleni, macho yangu yakakutana na msichana huyu wa kazi ambaye ni mwembaba kiasi ila aliye barikiwa sura nzuri yenye mvutu. Msichana huyu akaendelea na kazi zake na mimi nikaendelea kusimama hapa mlangoni.

“Diana hiyo tracksuit unaitafuta mwaka mzima?”

“Jamani kuna hili begi linanishinda kushusha juu ya kabati”

“Naruhusiwa kuingia?”

“Ingia tu”

Nikaingia ndani ya chumba cha Diana, ni chumba kizuri kilicho pangiliwa katika mpangilio mzuri na unao pendaza.

“Begi hilo hapo”

“Mmmm sasa unaweka vitu huku juu huitumii?

“Yaa si nimeacha mazoezi siku hizi nayo nikaona ni bora kuitupia huko”

Nikapanda juu ya kitanda kilichopo karibu na kabati hili la nguo, taratibu nikaanza kulishusha begi hili kubwa na nikaliweka kitandani huku nikihema kwani ni zito sana.

“Umeweka mawe ndani ama?”

“Yaani wee acha ni nguo tu hizo”

“Heee mbona zito sana?”

Diana akatabasamu tu huku akifungua begi hilo. Nikaona nguo nyinyi zikiwa zimepangwa vizuri. Akaanza kutoa nguo moja baada ya nyingine huu kwa mara kadhaa macho yetu yanagongana, na kuonyesha ishara ambayo kwa mtu muelewa wa haraka haraka kama mimi, ninaweza kufahamu kwamba kuna hisia fulani za kike ambazo zimesha anza kumsumbua Diana.

“Hizi bikini huwa unavaa?”

“Nilizungumza huku nikimuonyesha Diana moja ya bikini yake aliyo itoa kwenye begi.”

“Yaa nina vaa”

“Natamani nikuone ukiwa umevaa”

“Weee acha zako”

“Kweli au kuna tatizo?”

“Ndio tatizo lipo”

“Lipi?”

“Mimi na wewe tutabaki kuwa bosi na mfanyakazi wake”

“Mmmm, kwa sasa mimi sio bosi, ni kibaraka fulani tu mtaani”

“Wee hivi unahisi kwamba mama yako akihitaji kukutafuta huto rudi kweli kwenye himaya yake?”

“Sinto rudi kwa kweli na ataniua kwa jambo hilo”

“Hahaaa….hakuna kitu kama hicho?”

Kwa mabati mbaya Diana akaangusha moja ya nguo zake chini, kitendo cha kuinama ili kuokota nguo yake hiyo, mapaja yake yote yakaonekana kwa nyuma jambo lililo nifanya nisisimke na jogoo wangu akaanza kufurukuta furukuta ndani ya hili koti nililo jifunga. Diana akanyanyuka na kunitazama, ila kwa mshangao alio nikuta nao hata yeye mwenyewe akahisi nimeona kitu.

“Bosi….bosi”

“Yaa niambie”

“Mbona unashangaa umeona nini?”

“Ohoo…a..a….hamna kitu”

Nilizungumza huku nikijaribu kumbana jogoo wangu kwenye mapaja yangu, kitendo ambacho hata yeye mwenyewe aliweza kukishuhudia. Zoezi la kuendelea kutafuta nguo likaendelea taratibu huku kila mmoja akiwa kimya, kwa upande wangu hali inazidi kuwa mbaya kila ninapo tazama mwili wa Diana, siku zote alikuwa ni mfanyakazi wangu, niliishia kumtamani kwa macho na sikuhitaji kuweza kumueleza chochote, kutokana na tabia yangu kuwa mbaya, na wasichana kama Diana sio wa kutembea nao na kuwaacha, huwa wakipenda basi wanapenda kweli.

“Hii hapa”

Diana alizungumza huku akinikabidhi suruali pamoja na koti la tracksuit hii nyeusi, taratibu nikavipokea na kuzitazama vizuri.

“Asante”

Nilizungumza huku nikianza kutembea kueleka mlangoni.

“Unaniachia hili begi nilirudishe mwenyewe”

Kauli ya Diana ikanifanya nisitishe zoezi la kuelekea nje. Nikarudi sehemu alipo na nikaanza kumsaidia kurudisha nguo, ila muda huu mazungumzo kidogo yamekatika. Tulipo maliza kupanga nguo na kulifunga begi taratibu nikajitahidi kulinyua, ila kutokana na uzito, Diana akajumuika nami katika kulinyanyua na tukafanikiwa kulirudisha juu ya kabati. Kitendo cha kugeukiana kwa bahati mbaya kifua chake kikajibaraza kidogo kwenye kifua changu, na kutufanya tuwe kama watu tulio shikwa na bumbuwazi.

“Samahani”

Diana aliwahi kuzungumza huku akishuka kitandani. Nikamuwahi kumshika mkono wake wa kulia na kumvuta tena kitandani na kumfanya alale chali, tukatazamana kwa sekunde kadhaa, nikajaribu kumsozea mdomo wangu, ila akauzuia kwa kuniwekea kiganja mdomoni mwangu akiniashiria kwamba nisizungumze chochote.

“Sio sasa Randy, ninachelewa kazini”

“Sawa sawa”

Tartaibu nikashuka kitandani na nikatoka chumbani humu na kumuacha Diana akijianda ana kurudi kazini, kwenye kordo nikakuta na msichana huyu wa kazi, nikapishana naye huku na yeye akielekea chumbani kwa dada yake. Nikaingia chumbani kwangu na kuvaa nguo hizo nilizo pewa.

“Randy ninatoka”

Niliisikia sauti ya Diana, kwa haraka nikatoka na kumkuta akiwa amesimama mlangoni.

“Naomba usimuambie mtu yoyote sehemu nilipo sawa”

“Sawa, hata alex nisimuambie chochote”

“Ndio usimuambbie chochote”

“Sawa bosi. Dada utamsikiliza bosi anacho hitaji, kama atataka chakula muandalie”

“Sawa dada”

Diana akaondoka na kuniacha na huyu dada wa kazi ambaye kwa makadiria ya haraka haraka ana miaka kama ishirini hivi.

“Dada una simu?”

“Ndio kaka”

“Naomba uniazime”

“Ipo chumbani kwangu, ngoja niakuletee”

Dada huyu akaelekea chumbani kwake, akarudi akiwa ameshika simu ndogo ya kawaida tu. Nikampigia mkuu wa majeshi, simu yake ikaanza kuita na baada ya muda ikapokelewa. Nikajitambulisha na kumueleza kwamba nipo tayari kuungana na jeshi. Akaniomba mida ya saa mbili usiku nikaonene naye kwenye moja ya ukumbi wa starehe ili tuzungumze vizuri. Nikafuta namba ya mkuu huyo kisha nikamrudishia dada huyu simu yake. Mlango ukagongwa na dada huyu akafungua mlango wa sebleni, akaingia mwanajeshi ambaye kwa haraka haraka ninamfahamu ni mpenzi wake Diana. Akanitazama kwa macho makali na kunisogelea sehemu nilipo kaa.

“ Wewe mseng** umeona kutembea naye ofisini haitoshi leo umeamua uje kumtomb** mwanamke wangu hapa hapa kwake si ndio?”

Jamaa huyu alizungumza kwa ukali huku akinitazama, cha kushangaza zaidi ni pale alipo chomoa kisu kikubwa kidogo kwa ajili ya kunidhuru, jambo lililo nifanya nisimama kwa haraka ili kujiandaa kwa chochote ambacho kitakacho tokea kwa maana jaama anaonekana amedhamiria kunidhuru.


Kwa haraka nikasimama huku nikihamia kwenye sofa jengine huku nikimtazama huyu jamaa ambaye kwa haraka harakaisikia arufu ya pombe ikitoka kinywani mwake.

“Unazungumza ujinga gani wewe jamaa”

“Ujinga gani, umefwata nini nyumbani kwa mpenzi wangu”

“Huyu ni mfanya kazi wangu kuna matatizo yamenikuta na ameamua kunisaidia, sasa unacho kuudhi wewe ni nini, kama ningeamua kutembea naye si ningetembea naye nikiwa ofisi kwangu ehee?”

Ilibidi na mimi nije kuu kidogo huku nikimtazama jamaa huyu. Ila jamaa hukinielewa, akarusha kisu kwa bahati nzuri nikafanikiwa kukikwepa na nikamsindikiza na teke moja zito sana lililo msababisha kupepesuka na kuangukia meza hii ya kioo na ikavunjika yote. Kitu kilicho anza kutuchanganya mimi na huyu dada wa kazi ni mara baada ya kuanza kuona damu zikisambaa chini zikitokea katika kichwa cha jamaa huyu.

“Umeua!!!”

Dada wa kazi alizungumza huku macho yakimtoka, mapigo ya moyo yakazidi kunienda kasi sana kwani jaama hatingishi hata kidole, taratibu nikachuchumaa na kukinyanyua kichwa chake kwa nyuma, hapo ndipo nikagundua kuna kipande kikubwa cha kioo cha meza kimemchoma kwenye eneo la usogoni.

“Kaka umeua”

“Shiiii”

Nilizungumza kwa ukali huku nikimtazama mfanyakazi huyu usoni mwake.

“Naomba simu yako, na funga milango yote”

“Eheee?”

“Hujasikia au?”

Mfanyakazi huyu akaonekana kuweweseka kiasi cha kushindwa kutekeleza kile ninacho kihitai kwa muda huu. Kwa haraka nikakimbilia getini na kufunga geti kwa ndani, kisha nikarudi ndani na kufunga mlango kwa ndani.

“Simu yako”

Msichana wa kazi akanionyesha simu yake kwa ishara ya mkono ilipo, nikaichukua huku jasho jingi likinimwagika mwlini mwangu, nikaanza kuiandika namba ya Alex rafiki yangu wa karibu kabisa. Simu yake ikaanza kuita, baada ya muda ikapolewa.

“Alex, Alex nakuumba unisikilize kwa umakini”

“Randy”

“Ndio, nisikilize, ninakuomba umuambie Diana kwamba muje nyumbani kwake sasa hivi”

“Kuna nini kilicho tokea”

“Alex fanya hivyo, sina muda wa kujibu haya mambo”

“Sawa sawa, ngoja niende ofisini kwake na hii namba ni yako mpya?”

“Sio yangu nimeazima tu, hembu fanya uende ofisini kwake sawa”

“Sawa mkuu”

Nikakata simu huku nikimtazama jamaa huyu. Nikamtazama msichana wa kazi wa Diana, amekaa kwenye sofa huku mwili mzima ukimtetemeka kwa woga. Simu ya msichana huu ikanza kuita, nikaitazama na kukuta imeandikwa jina la dada D, kwa haraka nikaipokea na kuiweka sikioni mwangu.

“Halooo”

“Randy ni nini kimetokea, mbona Alex amekuja kunichukua juu juu?”

“Wewe fanya uje nyumbani sasa hivi”

“Randy una niogopesha hembu niambie ni kitu gani ambacho kimetokea bwana”

“Njooni haraka nyumbani”

Mara baada ya kuzungumza hivyo nikakata simu ili kuepuka kuzungumza kila kutu kwa maana ninaelewa kila mazungumzo ambayo tunayazungumza huwa yanarekodiwa kwenye mitandao jambo ambalo linaweza kuwa ushahidi mzuri sana pale askari watakapo anza kufanya upepelezi wao. Diana akapiga simu tena, nikaitazama kwa muda kisha nikaipokewa.

“Randy hembu niambie ni nini kinacho endelea hapo kwangu?”

“Diana mbona unakuwa sio muelewa, nimekuambia njooni nyumbani”

“Sawa tupo njiani, tunakuja, ila ni bora uniambie ni nini kinacho endelea, tafadhali nipo chini ya miguu yako Randy, ukiniacha hivi naweza hata nisifike huko nyumbani kwa presha”

“Ni kuhusiana na X boy friend wako bwana”

“Amefanyaje?”

“Sasa hayo ndio nisiyo yataka, wewe njoo hapa nyumbani”

Nikakata simu na kuizima kabisa. Dada wa kazi muda wote amejikunyanta huku mwili mzima ukiendelea kumtetemeka.

“Hei….hei…heiii”

Nilizungumza huku nikimuinamia msichana huyu wa kazi.

“Eheee

“Kuwa jasiri, hii iliyo tokea ni ajali sawa”

“Ehee”

Msichana aliendelea kuweweseka sana. Baada ya muda kidogo nikasikia honi ya gari getini, nikatoka nje huku nikitembea kwa hatua kubwa sana. Nikachungulia kwenye uwazi mdogo wa geti hili na kuliona gari la Alex, kwa haraka nikafungua geti na wakaingia ndani na gari hili. Nikafunga geti huku nikihakikisha kwamba nje hakuna mtu anaye fwatilia gari la Alex.

“Randy kuna kitu gani kinacho endelea?”

Alex aliniuliza mara tu ya kushusha kwenye gari.

“Kuna tatizo”

Nilizungumza kwa ufupi huku nikiwatazama wote wawili.

“Tatizo gani?”

“Diana alinuliza huku akionekana kuwa na shauku kubwa ya kuhitaji kufahamu ni kitu gani kinacho endelea.

“Boy friend wako alikuja hapa, akiwa amelewa, huku akiwa na kisu pamoja na nguo zake za jeshi”

Nilizungumza kwa hara haraka.

“Ohoo Mungu wangu, hajakudhuru jamani?”

Diana alizungumza huku akitetemeka mwili mzima.

“Alitaka kuniua na kisu chake”

“Oohoo jamani kwa nini anakuwa hivi, mimi na yeye si tulisha malizana jamani akhaa yupo wapi?”

Diana alitaka kuingia ndani ia nikamuwahi na kumzuia.

“Wewe baki kwenye gari, Alex twende ndani?”

“Jamani yule ninamjua mimi, acheni niendee kuzungumza naye atawadhuru”

“Kaa hapo na usiingie ndani”

Nilizungumza kwa ukali, huku nikimshika Alex mkono na kuanza kuelekea naye ndani. Kitendo cha kuingia sebleni, Alex akastuka sana baada ya kumkuta mpenzi wa Diana akiwa amelala chini, huku damu zikiwa zimesaambaa chini huku meza imepasuka pasuka.

“Randy hii ni nini?”

“Kama unavyo ona jamaa alihitaji kuniua, katika kumkwepa akaangukia meza na kwa bahati mbaya akaangukia meza na mambo yamekuwa kama hivi unavyo ona mwanangu”

“Daaa…..sasa tunafanyaje aisee”

“Sijui ndio maana ninakuita”

Alex naye akaonekana kuchanganyikwa, ukunga wa Diana ukatustua mara baada ya kuingia humu sebleni. Kwa haraka nikamfwata Diana na kumziba mdomo wake kwa nguvu.

“Ndio maana sikutaka uingie ndani humu”

“Niache bwana Randy”

Diana alijitoa kwa nguvu mikononi mwangu na kukimbilia katika mwili wa mpenzi wake. Akaendelea kulia huku akimtingisha kwa nguvu.

“Randy umefanya nini rafiki yangu”

Alex alilalama huku akinitazama usoni mwangu.

“Unahisi hapa nimefanya nini na wewe, eheee. Mtu anahitaji kuniua wewe unadhani ninge fanya nini”

“Randy toka ndani ya nyuma yangu na ninaita polisi”

Diana alizungumza kwa ukali hukua kitoa simu yake kwenye mfuko wa koti la suti yake.

“Acha upumbavu wewe”

Nikamfwata Diana sehemu alipo, nikaanza kuminyana naye ili aiachie simua liyo ishika. Dada wa kazi akaingilia kikiri kikiri hizi za kuhitaji kuhitaji kumpokonya dada yake simu na wakaanza kunishambulia kwa makofi mfululizo.

“Ehee kitua cha polisi hapo”

Sauti ya Alex ikanistua sana na kujikuta nikimtazama, nikamkuta akiwa ameiweka simu yake sikioni akijaribu kuwasiliana na askari. Kwa haraka nikamrukia na kuanza kuminyana naye huku nikiwa nimemshika koo lake.

“Kuna jambaz……ame……u….”

Alex alizungumza hukua kijitahidi walau kutoa taafira hayo ili mradi iwafike askari na simu yake bado ipo hewani. Diana na mdogo wake wakanisogelea na kunitoa mwilini mwa Alex ambaye kisawa sawa nimemng’ang’ania koo lake.

“Onge ongea”

Diana alizungumza huku akiminyana na mimi. Alex akapata upenyo wa kuzunumza na askari hao na kuwapa taafira, kwa haraka nikakimbilia kisu kilichopo chini na kukishika huku hukiwatazama.

“Sasa nina waambia endapo mtu atanishika, nitamchinja”

Nilizungumza huku macho yakinitoka, jasho likiendelea kunimwagika. Msaada ambao niliutarajia kuupata kwa marafiki zangu hawa, sijaupata na mwishowe nimeambulia kustakiwa polisi. Nikaanza kurudi nyuma hadi mlangoni, nikatoka na kuufunga mlango kwa nje, kisha nikaligagua gari la Alex na kukuta halina funguo. Sikua na jinsi ya kufanya zaidi ya kutoka nje ya geti na kuanza kukimbia nisipo pajua, kwani japo nimezaliwa katika nchi hii ya Nigeria, na nimeishi maisha mazuri, ila kuba baadhi ya mitaa hususani ya uswahilini siifahamu kabisa.

“Ehee Mungu ni nini hichi kilicho tokea kwenye maisha yangu”

Nilizungumza huku nikiwa nimejawa na wasiwasi mwingi sana, kila mara nikawa ni mtu wa kutazama nyuma kama kuna watu wanaweza kunifwatilia, ila sikuweza kuona chochote. Ili kupoteza ushahidi, nikaingia kwenye moja ya dula la nguo huku nikiwa na dola mia ambayo Diana alinipatia. Nikachagua suruali ya rangi ya kaki, tisheti nyeusi pamoja na swete lenye jikofia kubwa. Nikamlipa muuza duka, akanirudishia chichi yangu, nikabeba nguo zangu kwenye mfuko na kuanza kutembea mitaani. Nikafika kwenye moja ya kichochoro nikavua nguo zangu zote kisha nikavaa hizi nyingine na kuendelea na safari yangu ya kujiwinda huku akilini mwangu nikiwa na wasiwasi mwingi sana, kwa maana mtu niliye sababisha kifo chake, kwanza ni mwanajeshi halali wa hii nchi, pili ni mpenzi wa Diana sekretari wa kitengo nilicho kuwa ninakifanyia kazi na dhairi inaonyesha Diana ana mpenda mpenzi wake, hata kama wamegombana na kudai kwamba wameachana.

Hadi giza linaingia, likanikuta mtaani huku nikiwa nimechoka na njaa kali ikinisumbua tumboni mwangu. Ahadi ya kukutana na mkuu wa jeshi kidogo ikanipa mashaka, kwa maana nimemua kijana wake japo ni kwa bahati mbaya ila ni lazima nitaonekana ni muhalifu. Nikafika kwenye baa ambayo nilipanga kuonana naye majira haya ya usiku, kwa jinsi ambavyo nime vaa ni vigumu sana kwa mtu ambaye ananifahamu kuweza kunifahamu. Hazikupita hata dakika kumi, gari nyeusi aina ya Hammer, ikafika katika baa hii, akashuka mkuu huyu wa majeshi huku akiwa ameongozana na vijana wake wawili walio valia sare za kijeshi japo yeye amevalia nguo za kiraia. Nikajibanza kwenye moja ya nguzo ya baa hii, huku nikiendelea kumtazama anavyo tembea kuja katika sehemu hii, akatazama tazama kila sehemu kisha akaa kwenye moja ya kiti.

‘Nenda hato kufaya jambo lolote’

Nilijifariji kimoyo moyo huku nikiendelea kutazama mazingira ya eneo hili. Nikatembea kwa kujiamini hadi kwenye meza ambayo amekaa, nikavuta kiti na kukaa.

“Shikamoo muheshimiwa”

Nilimsalimua huku nikivua kofia hili la sweta nililo vaa.

“Kwa nini umemuua kijana wangu?”

“Hapana muheshimiwa sijamuua kijana wako, na laiti kama ningemuua mimi wala nisinge kuja. Ila ile kesi wame ni frame”

Mkuu huyu wa majeshi akanitazama kwa muda jinsi ninavyo zungumza kwa kujiamini.

“Mimi sio mtu wakupindisha pindisha maneno. Jeshini huwezi kuchukuliwa kwa sasa kwa maana ni muhalifu na muhalifu ni lazima afikishwe mbele ya vyombo vya sheria na wewe hivi sasa ndipo unapo takiwa kwenda hivyo. Vijana wangu watakuchukua na kukupeleka katika vyombo vya sheria na endapo utafanya fujo yoyote basi ni lazima watakuua, hatuto jali kwamba mama yako ni tajiri au tumeingia naye mikataba gani ili kusaidia taifa umenielewa?”

Maneno ya mkuu huyu wa jeshi yakaanza kunitetemesha mwili mzima, vijana wake walio simama pembeni yake, wakanionyesha bastola zao kwa kuyafunua mashati yao katika maeneo ya kiunoni walipo zichomeka.

“Dili mimi na wewe limekwisha, mkamateni na mumpeleke kwenye gari”

“Mkuu nakuomba unisikilize”

“Nikusikilize vipi ikiwa umemuua kijana wangu na yule alikuwa anaelekea katika rank za kuwa komandoo, wewe umemuua, huoni kwamba umelitia taifa hasara?”

Mzee huyu alizungumza kwa ukali ila kwa sauti ya chini yenye msisitizo mkubwa sana.

“Nakuomba unipatie japo dakika moja niweze kujielezea jinsi tatizo lilivyo tokea.”

“Hakuna muda huyo, mkamateni na mumpeleke kwenye gari na hakikisheni kwamba munamuua kimya kimya.”

Vijana wake kwa haraka wakanikamata magekani mwangu, wakaninyanyua kwa nguvu na kuwafanya watu wote ndani ya hii baa kujawa na mshangao. Wakaninyanyua mkuku mkuku hadi ndani ya gari hili walilo kuja nalo, wakapanda ndani ya hili gari kisha dereva tuliye mkuta ndani ya gari hili akaanza kuendesha.

“Jamani nambeni mu……”

Nikahisi kimlio fulani kikali sikioni mwangu kilicho tokana na kupigwa kisukusuku kizito na mmoja wa wanajeshi hawa walio niweka katikati. Wakatoa bastola zao, mmoja akaniwekea kwenye mbavu huku mwengine akiniwekea bastola yake kwenye paja. Maumivu ambayo ninaendelea kuyasikilizia kwenye sikio langu la upande wa kulia kusema kweli ni makali sana. Gari hili likaendeshwa hadi kwenye moja ya msitu, nikashushwa na kuanza kupatiwa kipondo kikali sana, na hakika kile alicho kizungumza mku huyu wa jeshi, hakika ndicho vijana wake wanacho kwenda kukifanya, nikajaribu kufa kiume japo kwa kurusha ngumi kadha, ila nikajikuta nikishindwa, kwani jamaa ni wakakamavu na wenye mafunzo mazito ya kijeshi.

Kadri jinsi wanavyo zidi kuendelea kunipiga kipigo kizito ndivyo nilivyo anaza kuiona sura ya mama yangu katika matukio mbalimbali, tukio la furaha ni lile alilo weza kunizawadia gari la kifahari siku ya kutimiza miaka ishirini na mbili. Nikamuona kijana mmoja akikoki bastola yake huku akinitazama kwa sura ya hasira, akanielekezea bastola yake hii, mmoja akanichomoa na wakaanza kunikokota kwa hadi kwenye ukingo mrefu wa majabali yam awe huku chini kukiwa na mto mkubwa wa maji.

“Sogea hapo”

Jamaa aliye shika bastola alizungumza na mwenzake akaniachia, kwa jinsi walivyo nipiga, nikakosa hata muhimili wa kusimama na nikajikuta nikipiga magoti chini na kuwatazama. Nikasikia mlio wa bastola hiyo huku nikihisi kitu cha moto kikiingia kwenye kifua changu, nikajikuta nikiweweseka na mwisho nikaanza kuelea angani huku nikipiga kelele, kwani ninapo elekea chini katika mtu huu, hakuna stori nyingine zaidi ya kufa tu.



Nikadumbukia kwenye maji mengi haya ya baridi, yakaanza kunisukuma kwenda mbele, kadri muda jinsi unavyo zidi kwenda ndivyo jinsi nilivyo jikuta nikipoteza nguvu na baada ya muda nikajikuta nikipoteza fahamu.

***

Milio ya mbuzi na kondoo, ikanifanya nifumbua macho yangu taratibu. Mwanga mdogo unao ingia kwenye eneo hili, ukanisaidia kuona vitu vilivyomo katika chimba hichi kidogo. Kitanda nilicho lalia kimetengenezwa na kamaba, nikajitazama kifuani mwangu na kukuta nikiwa nimefungwa na bandeji kubwa huku mwilini mwangu nikiwa na suruali tu ambayo niliinunua. Taratibu nikajitahidi na kukaa kitako kitandani. Nikashusha pumzi taratibu huku nikitazama chumba hichi ambacho kuta zake zimetengenezwa kwa matofali ya kuchoma. Wakaingia watoto wawili wadogo wakiume wakicheza cheza, nikasikia sauti ya kike ikizungumza, akaingia mwanamke aliye valia baibui huku amejifunika uso wake vizuri na kubakisha macho yake tu.

“Asalam alykum”

Alinisalimia huku akinitazama.

“Walyakum mslamm”

Nilijibu kwa upole sana huku nikimtazama yeye na hawa watoto ambao alikuja kuwatoa humu chumbani kwa madai ya kwamba kuna mgonjwa na nisisumbuliwe. Akawanong’oneza watoto hawa, kisha wakatoka nje na wakaendelea kucheza michezo yao.

“Unajisikiaje na hali?”

“Kidogo afadhali, nimefikaje hapa?”

Dada huyu akachungulia nje kidogo kwa kufunua pazia lililopo katika mlango wa chumba hichi. Taratibu akarudi na kukaa kwenye moja ya stuli ya mbao ni chakavu kidogo.

“Mume wangu na vijana wake wachungaji walikuokota kwenye ziwa Niger ukiwa umepoteza kumbukumbu huku ikiwa na majeraha mwilini mwako, ikiwemo hilo jeraha la risasi kifuani mwako”

Dada huyu kusema kweli ana sauti nzuri sana, kiasi kwamba amenifanya nishikwe na kigugumizi hata cha kuendeea kumshukuru kwa msaada walio weza kunifanyia.

“Mume wangu atarudi muda si mrefu, ngoja nikuandalie kifungua kinywa”

“Sawa”

Mwamke huyu akatoka ndani humu na kuniacha nikiwa nimekaa kitandani, nikajitaza mwili wangu, na kuona jinsi nilivyo jeruhiwa kwenye baadhi ya maeneo ambayo yalitokana na kupigwa na wale wanajeshi. Kama nimeokotwa kwenye mto Niger, basi nipo katika nchi hii ya Niger ambao ni majirani zetu na nchi ya Nigeria. Taratibu nikanyanyuka kitandani na kutoka nje, nikaona nyumba nyingi zilizo jengwa kwa matofali ya kuchomwa. Watu wengi katika eneo hili wamevalia kanzu na baibui, mavazi yanayo ashiria kwamba watu wanao kaa hapa wengi wao ni waislamu wenye msimamo na dini ya kiislamu. Mzee mmoja marefu mweusi kidogo na mwenye ndevu nyingi kidevuni mwake, akanifwata katika eneo hili nilililo simama huku akiwa na sura ya tabasamu kidogo. Nikamsalimia kwa heshima kidogo huku nikiinamisha kichwa changu chini kidogo.

“Unajisikiaje kijana”

“Salama mzee”

Mzee huyu akanitazama jeraha langu la kifuani, kisha akatingisha kichwa kidogo akionyesha ameridhika na maendeleo ya kidonda changu.

“Katika siku chache kitakauka”

“Ni kweli”

“Karibu huku”

Alizungumza mzee huyu na tukaeleka katika nyumba nyingine ya pembeni na hii nyumba niliyopo. Tukaingia sebleni na kukaa katika kapeti lilo tandikwa chini vizuri.

“Nahisi mke wangu mdogo atakuwa amekueleza jinsi tulivyo kusaidia?”

Hapa ndipo nikagundua kwamba mzee huyu ndio aliye nisaidia yeye na wanae.

“Ndio alinieleza kwa ufupi, ila ninashukuru sana mzee wangu kwa kuweza kunisaidia katika yote hayo”

“Usijali ni jukumu kwa binadamu kuweza kusaidiana. Hivi unaitwa nani?”

“Ninaitwa Randy”

“Umetokea nchi gani?”

“Nigeri”

“Ohoo ni kama vile nilivyo kuwa nimehisi, ni nini kimekupata kijana?”

Nikakaa kimya kwa muda kidogo huku nikitafakari kile ambacho nitokea.

“Nilivamiwa na majambazi, walinipora gari langu na pesa kisha wakanipiga risasia na kuanzai hapo sikufahamu ni kitu gani kinacho endele”

“Aisse pole sana kijana, dunia kwa sasa imekwisha, ni siku ya pili toka uwepo hapa nyumbani kwangu, tulivyo kulete siku ya kwanza hali yako kwa kweli ilikuwa ni mbaya sana hadi mke wangu alihisi kwamba hauto pona, ila mwenyezi Mungu amekusaidia umepona kwa kweli ni jambo la kumshukuru Mungu”

“Ni kweli kabisa, Mungu ni mwema”

“Mimi ninaitwa Mzee Khalid, nina watoto wangu wanne, wote ni wa kiume. Wakubwa wawili wapo wanachunga kondoo na mbuzi huko nyikani na nina mapacha wawili wapo jikoni na mama yao”

“Hongera sana mzee wangu”

“Nashukuru, vipi wewe una mke au mtoto?”

“Hapana sina”

“Sawa sawa, inabidi utafute bwana”

Mzee Khalid alizungumza kwa utani kidogo, mke wake aiangia huku akiwa ameshika chupa ya chai pamoja na sahani yenye viazi vinavyo fuka mvuke wa moshi. Akatuwekea, kisha akatoka humu sebleni, baada ya muda kidogo akarudi akiwa ameshika vikombe viwili pamoja na bakuli lenye maji . Akatumiminia maziwa haya, na akatunawisha maji na kutoka ndani humu.

Taratibu tukaanza kupata kifungua kinywa na mzee huyu ambaye amekuwa mcheshi sana kwangu. Mzee Khalid akanihadithia mambo mengi sana yanayo endelea katika mji huu unaoitwa Agadez, ambao ndio mji wao mkuu wa nchi hii.

Siku zikazidi kusonge mbele huku nikiwa ninaendelea kuugua majeraha yangu nikiwa nyumbani kwa mzee Khalid, kwa kipindi hichi kifupi nilicho kaa nao nimekuwa kama mwana familia ambaye nimetokea kupenda sana na kila mtu. Mzee Khalid akatuomba mimi na vijana wake, tuongozane naye kwenye mkutano unao husinaa na wanaume tu katika mji huu ambao unafajika majira haya ya jioni.

“Kuna ajenda gani ambazo zitazungumziwa kwenye kikao hicho?”

Nilimuuliza mzee Khalid mara baada ya kumaliza kujiandaa, kuvaa kanzu yangu nyeupe pamoja na kobazi.

“Hatujafahamu ila nina imani kitakuwa ni kikao muhimu sana”

“Sawa”

“Wezako vipi wamesha jiandaa?”

“Ndio mzee wangu”

Tukatoka sebleni na tukaanza safari ya kuelekea katika uwanja ambao utatumika kwa kikao hichi. Tukafika katika kiwanja hichi na kukuta baadhi ya wanaume wakiwa tayari wamesha kusanyika. Tukatafuta sehemu nzuri yenye nyasi nyingi kidogo, nikakunja kanzu yangu kisha nikaka chini huku nikiwa nimeikalia suruali yangu. Baada ya muda kidogo gari zipatazo kumi za jeshi zikazunguka kiwanja hichi jambo lililo nistua sana, nikatamani kunyanyuka ila mzee Khalid akanishika mkono.

“Tulia hawa ni watu salama tu kwetu”

Mzee Khalid alizungumza huku tukkitazama kundi kubwa la wanajeshi wenye silaha wakishuka katika eneo hili huku wakiwa wameshika silaha zao mikononi.

“Salama kivipi ikiwa wanazunguka kiwanja kama wanatutuka?”

“Hapana hakuna ambaye atatekwa”

“Hawa ni wanajeshi wa serikali au wanajeshi gani?”

“Hapana hili ni jeshi ambalo linapigania Uislam, hapo awali lilikuwa nchini Nigeria, lilikuwa linaitwa Boko Haramu, ila kwa sasa haliiti hivyo na limehamishia makazi yake hapa Niger”

“Sasa kwa nini wapo hapa?”

“Wamekuja kuzungumza nasi”

Kusema kwelia amani yangu yote ikanitoweka, nikajikuta nikiwa makini sana kuwachunguza wanajeshi hawa. Akashuka mkuu wao kwenye moja ya gari na akatembea hadi kwenye viti vilivyo andaliwa na viongozi wa wanachi, akakaribishwa kwa heshima kisha akaka. Kiongozi wa mji akatusalimia salamu iliyo itikiwa na wanaume wote ila kasoro mimi tu, hii ni kutokana na amani kunitoweka mooyoni mwangu.

“Jeshi letu linahitaji vijana wengine, ili tuweze kujihimairisha”

Mkuu wa jeshi hili alizungumza huku akiwa amesimama. Kilicho zidi kunishangaza ni watu kuanza kupiga makofi wakionekana kushangilia kwa kile alicho kizungumza mkuu huyu wa jeshi, hata watoto wa mzee Khalid nao wanaonekana kujawa na furaha sana kwa kauli hiyo.

“Leo tutachagua vijana mia moja, na kesho alafajiri waweze kuhudhuria bila kukosa kwenye kiwanja hichi na endapo itatokea, mtu akakimbia basi kitakacho tokea kwa kijana huyo na familia yake basi tusilaumiane, kikubwaa ni kuhakikisha wazee muna walinda vijana wenu na muhakikishe kwamba kesho wanafika bila ya kukosa sawa”

Watu wakaendelea kuitikia kwa furaha ambazo kwa namna moja ama nyingine ni unafki tu moyoni mwao na wengi wao kwenye mioyo yao hawana furaha. Mkuu huyo wa jeshi akasimama na kuaomba vijana wote tusimame, taratibu tukasimama tukaamrishwa kusimama kwenye mistari miwili iliyo nyooka. Akaanza kutupita katika ya mstari huu huku akitukazia macho. Akaanza kuchangua mmoja baada ya mwengine, akafika kwangu, akanitazama vizuri kwa muda wa kama dakika moja, kisha akanichagua na akaendelea na wengine. Ilipo timia idadi ya vijana mia moja tukatenganishwa na vijana wengine ambao bado hawajachaguliwa.

“Nyinyi kuanzia sasa ni wanajeshi, wanajeshi ambao mutasimama kwa ajili ya kupigania haki ya dini yetu, haki ya kuhakikisha tunajitambua sisi ni kina nani na tuna misingi gani kwenye jamii hii”

Mkuu huyu wa jeshi alisimama huku akipita katikati ya mistari minne tuliyo panga.

“Leo usiku ndio utakua usiku wenu wa mwisho wa kulala nyumbani kwenye vitanda vyenu. Kuanzia kesho alfajiri utakuwa ni muda wa nyinyi wa kuzaliwa upya na kuwa wanaume. Wanaume watakao kuwa tayari kufa kwa ajili ya haki ya watoto wao takakao kuja kurithi hili tunalo lifanya”

Mkuu huyu alizungumza huku akinitazama kwa umakini sana hadi watu wengine wakabaki wakinitazama. Tukaruhusiwa kurudi kwenye sehemu zetu, kisha mkutano ukaendelea kwa muda kidogo, kisha wanajeshi hawa wakaondoka na kutuacha wananchi tukitawanyika kila mmoja kurudi nyumbani kwake.

“Mzee wangu hadi sasa hivi ninashindwa kuelewa, ni kitu gani kilicho wafanya mushangilie wanajeshi hawa”

Nilimuuliza mzee Khalid huku tukiwa njiani tukirudi nyumbani.

“Shiii…hili swala Randy tutalizunumza tukiwa nyumbani”

“Randy kwani hujafurahi kuchaguliwa?”

Hassan mtoto wa mzee huyu aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.

“Sijafurahi ndio”

“Haa tunakwenda kuwa mashujaa”

Hussein alichangia naye mada kwani sote tumechaguliwa kuweza kuwa katika kikisi hichi.

“Ushujaa wetu hapo ni upi, kufunzwa mafunzo ambayo hayana msingiwala msaada wowote kwenye haya maisha yetu”

Maneno yangu yakawafanya wazee wawili alio tangulia mbele yetu kugeuka nyuma na kunitazama kwa mshangao mkubwa sana.

“Randy”

Mzee Khalid aliniita huku akinitazama kwa macho yenye ishasha ya kuniomba nikae kimya nisiendelea kuzungumzia mada hii. Tukafika nyumbani na moja kwa moja tukapitiliza sebleni, tukamkuta mke mdogo wa mzee Khalid akiwa amekaa na wanaye wakitazama tv ndogo. Mama akamsalimia mume wake kwa heshima, kisha akatoka sebleni hapa.

“Randy nahisi kwamba hukuufahamu utaratibu wa hapa. Kila mwaka tarehe kama ya leo, jeshi huja kuchukua vijana ambao wanakwenda kujiinga na jeshi lao, wanapata mafunzo maalumu na wanakuwa ni wanajeshi mahiri”

“Na faidi ya kujiunga na jeshi hilo ambalo sio la serikali, ni nini haswa?”

“Ni usalama wa raisi, usalama wa familia. Kwa mfano wewe ukakimbia basi hii famili nzima inakwenda kuuwawa na wewe watakusaka nchi nzima na watakusaka, je upo tayari sisi tufe kutokana na kukataa kwako?”

Swali la mzee Khalid likanifanya nikae kimya kidogo huku nikimtazama usoni mwake.

“Randy wewe ni sawa na mwanangu, ninakuomba sana usije ukafanya jambo lolote ambalo litaifanya familia yangu kuwa katika wakati mgumu. Tumeishi na wewe hapa kwa miezi mitatu, hatujawahi kukuonyesha ishara yoyote mbaya ya kuto kukupenda. Hembu ungana na wezako kesho, ili kutuweka mimi na wake zangu na hawa vijana wadogo kwenye hali ya usalama. Umenielewa mwanangu?”

Nikashusha pumzi taratibu.

“Najua hujapenda Randy na nilikupeleka wewe pasipo kukueleza ukweli, ila ninakuomba uweze kunisamehe katika hilo na laiti kama ningekuacha hapa nyumbani, wangetuma jeshi kuja kukagua na mwisho tungepewa adhabu moja kali sana nakuomba sana mwanangu”

“Nimekuelewa mzee”

Mzee Khalid akatabasamu, kisha taratibu akanikumbatia.

“Tutaanza kuwafanyia maandalizi machache ya nguo na chakula”

“Mimi sinto hitaji mupate tabu kwenye hilo swala la maandalizi, labda muwaandalie Hassan na Hussein”

Baada ya kuzungumza maneno hayo nikanyanyuka na kutoka sebleni humu, nikamuta mama akiwa nje amesimama akisikiliza mazungumzo yetu. Nikampita pasipo kuzungumza kitu chochote, nikaelekea chumbani kwangu na kujifungia ndani huku nikiwa nimejawa na mawazo mengi sana.

‘Nitoroke…….? Hapana mzee wa watu anaweza kuuwawa na watoto wake hawa wadogo’

Niliwaza kimoyo moyo. Nikayakumbuka maisha kitajiri niliyo kuwa nikiishi nyumbani kwa mama yangu, japo amani kidogo ilikuwa ni tete, ila shida ndogo ndogo hazikuwepo nyumbani kwetu. Kitendo cha mkuu wa majeshi alicho nifanyia kikaanza kujirudia kichwani mwangu, nikawakumbuka Diana na Alex jinsi walivyo nisaliti na kuhitaji kunikamatisha mikononi mwa askari kwa kosa ambalo lililotokea bahati mbaya. Nikamkumbuka maneno ya mama yangu ya kuhitaji niwe jasiri ili aweze kunieleza ukweli kuhisiana na baba yangu.

‘Lazima nifanye kitu, lazima niwe Randy mwanaume na si Randy wa sasa’

Nilijiapiza kimoyo moyo huku nikiendelea kujilaza kwenye kitanda changu hichi. Usingizi yaratibu ukaanza kunipitia, na nikalala usingizi fofo.

Mpaso wa usoni mwangu ukanifanya nifumbue macho yangu kwa haraka, nikamkuta mama akiwa amekaa pembeni ya kitanda hichi.

“Sa…sa…mahani Randy….nimekuja kukuamcha ukapate chakula kwa maana wezako wamesha kula”

Mama alibabaika huku akiweka chini taa ya chemli. Tartaibu nikaka kitandani huku nikimtaza machoni mwake, kwani tangu nije kwenye hii nyumba sijawahi kuiona sura yote ya huyu mama ambaye ni mke mdogo wa mke wa mzee Khalid, na leo kulikuwa na taarifa kwamba mke mkubwa wa mzee huyo anarud hapa nyumbani.

“Saa ngapi sasa hivi?”

“Ni saa saba kasoro usiku”

“Mbona umekuja huku muda umekwenda?”

“Randy nimekuonea huruma sana, naumia kukuona unalala bila ya kula na huko unapo kwenda ni sehemu ngumu sana, sehemu yenye mateso ambayo asilimia kubwa ya vijana walio kwenda huko wengi hawarudi wakiwa hai”

Maneno ya mama yakaanza kuniogopesha.

“Jeshi lile sio la kupigania haki, ni jeshi la kupigania maslahi ya kiongozi wao. Niilipoteza ndugu zangu, wadogo zangu, baba yangu kwa ajili ya jeshi hilo. Niliolewa bado mdogo sana Randy kutokana sikuwa na pa kwenda, nilikuwa na ndoto kubwa sana. Ila zote zilikatishwa na hao washenzi wanao sema wanapigania haki”

Mama lizungumza huku machozi yakimlenga lenga. Taratibu nikashuka kitanda, kwa ishara nikamuomba anisubirie humu ndani, nikatoka nje na kuanza kuchunguza eneo hili zima, sikumuona mtu wa aina yoyote na katika dirisha la chumba cha mzee Khalid nikasikia akikoroma kwa usingizi. Nikarudi chumbani kwangu na kuufunga mlango kwa ndani uzuri chumba changu kimejitenga na nyumba kubwa.

“Ehee niambie ilikuwaje mama?”

Mama akaanza kuminya minya vidole vya mikononi mwake.

“Randy ninakuomba usiniite maana, mimi ni mdogo sana kuliko hata wewe”

“Una umri gani?”

“Miaka ihirini na moja”

“Kweli?”

“Haki ya Mungu vile”

Mama taratibu akafungua kitambaa alicho jifunika usoni mwake, nikajikuta nikiwa nimeshikwa na bumbuwazi moja zito, kwani uzuri wa sauti yake unaendana na uzuri wa sura yake. Ni mwanamke mwenye asili ya kiarabu, sura yake imebarikiwa kila sifa ya kuitwa mwanamke mwenye sura nzuri.

“Randy mimi bado ni mdogo, nimeolewa na mwanaume huyu nikiwa sina jinsi tu, amenizalisha watoto wale nikiwa na miaka kumi na nne. Randy ninakuomba unisaidie kutoroka kwenye maisha haya nakuomba unisaidie kuishi mbali mimi na wanangu. Najua nikiwa mbali na nchi hii ninaweza kulipiza kisasi cha familia yangu iliyo uliwa na wale wana haramu”

“Mmm huo mtihani ulio nipa ni mgumu sana mama”

“Randy niite Farida, usiniite mama”

“Sawa Farida, kumbuka kwamba mimi hapa muliweza kunisaidia kwa wema, inakuwaje nikutoroshe huoni nitatengeneza chuki na huyu mzee”

“Simpendi huyu mzee hususani huyu mke wake mkubwa aliye kuja leo, nakuomba Randy, ondoka na mimi hata muda huu, nipo tayari kwenda kuwachukua watoto wangu na tutoroke usiku huu. Ukiniacha hapa nitakufa Randy mimi na wanangu”

Maneno ya Farida yakanipa wakati mgumu na wasiwasi mwingi kwani tayari mzee Khalid alisha niomba niweze kujitolea kwenda kujiunga na jeshi hilo la waasi, ili maradi niiokoe familia yake, ila Farida naye anataka nimsaidie ili kumuokoa kutoka kwenye kifo yeye na wanaye, maombi yanayo niweka njia panda na ninashindwa nimsaidie nani kati ya Farida na wanaye au mume wake na familia nzima.



Farida akanishika mashavu yangu na kukigeuzia kichwa changu usoni mwake.

“Randy ninakuomba, tafadhali, kuja kwako kwenye hii nyumba kumenifanya niishi kwa amani, vipigo vya mzee huyu nimevisaahau, najua anaishi maisha ya kuigiza kwa ajili yako”

Farida alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake. Taratibu nikaishusha mikono yake kutoka kwenye mashavu yangu na kuishika vizuri.

“Kukusaidia ninaweza, ila siifahamu hii nchi vizuri, sijui ni wapi nitaanzia katika kukutorosha?”

“Mimi nina ramani ya nchi hii yote”

“Kuwa na ramani sio sababu, ni lazima tuweze kupata watu wanao weza kutusaidia kutoka katika hii nchi kwa siri sana, la sivyo tunaweza kukamatwa na kuuwawa”

“Randy nakuambia ukweli, ukikubali kwenda huko ni lazima utauwawa, nyinyi ndio mutakuwa munatolewa chambo kwenda kupigana na majeshi ya serikali, ya Nigeria, au kuvamia sehemu nyingine ambapo mwisho utajikuta unakufa”

Farida aliendelea kunishawishi huku machozi yakimwagika usoni mwake.

“Unaweza ukanipa wiki moja nikaenda huko kisha nikatoroka na kuja kukusaidia?”

“Sijawahi kusiki mtu ametoroka kwenye kambi ya watu hao na akaachwa hai”

“Usijali, nitahakikisha kwamba nina toroka, sawa Farida?”

“Kweli Randy unaniahidi?”

“Nakuahidi niamini mimi”

Farida akanikumbatia kwa nguvu huku machozi yakiendelea kumwagika usoni mwake. Maziwa ya Farida yakaanza kunipapasa kifuani mwangu, kwa jinsi nilivyo jawa na hamu ya kukutana na mwanamke, taratibu nikaanza kuhisi jogoo wangu akifurukuta kwenye suruali yangu. Nikajikuta nikiushusha mkono wangu ulio kuwa umemshika mgongoni mwake, hadi kwenye kiuno chake, taratibu nikakitomasa taratibu na Farida hakutikisika wala kuutoa mkono wangu. Nikaendelea kukitomasa kiuno chake huku tukiwa tumekumbatia, kilioa cha Farida kikabadilika na kuwa kilio cha miguno ya kimahaba.

Msisimko wa mapenzi ukazidi kupanda na nikajikuta nikisahau kwamba huyu ni mke wa mtu na hapa ni lipo ni nyumbani kwa mume wake. Taratibu nikamlaza Farida kitandani na nikaanza kuyatomasa maziwa yake yaliyo simama kana kwamba hajawahi kunyonyesha mtoto hata mmoja. Nikausogeza mdomo wangu karibu kabisa na lipsi zake, nikataka kumnyonya, ila nikakikuta nikisita, kwa ni shuhuli yangu nina ijua na Farida kama yeye hato weza kunitosheleza na anaweza kunisababisha matatizo ambayo kwa sasa ninaweza kuyaepuka.

“Samahani”

Nilizungumza huku nikimuachia mwili wake, nikaa vizuri kitandani na yeye akanyanyuka huku hukiwa amejawa na aibu kubwa sana.

“Samahani kwa hili”

“Usijali Randy”

Farida alizungumza huku akianza kujifunga ushungi wake kichwani, akaziba vizuri uso wake, akaokota taa yake ya chemli na kutoka chumbani humu na kuniacha katika hali tete kwani, tayari baba yangu alisha jiandaa kwa ajili ya mashambulizi, ambayo natambua kwa bingiri bingiri ambazo ningempatia Farida hakika mume wake na watoto wake wangeamka ili kusikilia ni nini kinacho endelea chumbani kwangu. Sikupata usingizi kabisa, zaidi ya kuendelea kufiria maisha yangu haya ya sasa hivi ambayo kusema kweli yamepoteza dira.

Nikatoka nje ya nyumba hii na kunza kutazama mwanga wa mbala mwenzi, inayo angaza vizuri katika eneo hili, kwa mbali nikaanza kuhisi njaa, nikaingia sebleni na kuchukua hotpot lenye chakula changu kisha nikatoka ndani humu.

Nikaanza kula taratibu huku mawazo yakizidi kunitawala kichwani mwao.

“Unakula sasa hivi?”

Sauti ya mzee Khalid ikanistua kidogo na kunijikuta nikimtazama akitoka kwenye mlango wa sebleni, kwa maana nimekaa nje.

“Yaa, nililala bila ya kula”

“Sawa sawa, naona umejiandaa kwa ajili ya kesho?”

“Sio kesho ni leo alfajri”

“Kweli, ila ninashukuru sana Randy”

“Kwa nini?”

“Kwa kubali kujuimuika na jeshi lile?”

“Usijali mzee wangu, unajua wewe sasa umekuwa kama baba yangu. Hivyo sina budi kama mtoto kuweza kumsaidia baba kwenye msaada ambao ni bora na familia”

“Ni kweli sana, ila ninakuomba ukiwa huko ninakuomba uweze kuwatazama hawa ndugu zako, kuwa japo mtetezi wao endapo kuna mambo mambo ya uonevu yatatokea”

“Sawa sawa mzee wala usijali katika hili”

“Inabidi kabla ya kuondoka nikutambulishe kwa mama yao mkubwa kwa maana amekuja na hujaona naye”

“Ahaa…sawa sawa baba”

Nikaendelea kupata kifungua kinywa taratibu hadi nikamaliza, nikarudi chumbani kwnagu, kusukuma sukuma saa ili marafi muda wa kuondoka utakapo fika, niweze kuondoka.

Masaa kwa kweli kwa siku ya leo yamekwenda kasi, kwani muda wa kuondoka umefika haraka sana. Nikatoka chumbani kwangu, nikawaka Hussein na Hassan wakiwa nao tayari wamesha maliza kujianda huku wakizungumza na mma yao pamoja na baba yao.

“Randy huyu ndio mama Hassana na Hussein niliye kueleza jana usiku”

“Ahaa, habari yako mama”

“Salama tu”

“Huyu ndio yule kijna niliye mpatia msaada, kusema kweli ni kijana msikivu mnyenyekevu na muelewa”

“Karibu sana kwenye familia yangu”

“Nashukuru sana mama”

“Ninakuomba ukawe muangalizi wa wezako huko mendapo, nina amini kwamba mwenyezi Mungu atawasimamia na mutapambana kwa haki ya jina lake”

“Sawa mama”

Nikamuona Farida akitoka chumbani kwake, akasimama kwenye mlango wa chumba chake kwa muda kidogo huku akionekana kujawa na masikitiko makubwa sana. Akatusalimia, nasi tukamsalimia kwa heshima zote kama siku zote. Katika kupena naye mikono akanikabidhi karatasi aliyo ikunja vizuri sana, kwa siria sana pasipo mtu wa aina yoyote kuweza kufahamu.

“Ujiangalie wewe na wezako”

Farida alizungumza kwa upole huku akinitazama usoni mwangu.

“Nashukuru”

Akaingia chumbani kwake na kutuacha hapa sebleni, baada wazee kutuhusiana mambo mawili matatu tukatoka nyumbani hapa na kuanza safari ya kueleeka katika uwanja ulio fanyika mkutana siku iliyo pita. Tukafika kiwanjani na kuwakuta vijana wengine ambao walichaguliwa jana wakiwa wamesimama huku kila mmoja akiwa na begi lake. Mimi peke yangu ndio kidogo sina hata kifuko. Barua hii aliyon nipatia Farida, nikaiingiza katikati ya mkanda wangu wa suruali ambao kidogo umechanika. Haukupita muda mwingi sana, gari za jeshi zikafika katika kiwanja hichi, wakashusha wajeshi wenye silaha huku wakiwa wameongozana na kiongozi wao.

Tukaamrishwa kupanga mstari mmoja kisha, tukaanza kuhesabiwa namba na kila mmoja akakaidhiwa namba yake, huku mimi namba yangu ikiwa ni ishirini na sita. Tukaingiangia kwenye lori moja watu ishirini, huku wengine wakiingia kwenye malori mengine.

“Wewe shuka”

Mkuu wao alinionyeshea kidole, taratibu nikashuka, akaendelea kunitazama kwa umakini sana, kisha akanionyesha nikaingie kwenye gari lake aina ya Jeep. Baada ya mambo yote kukamilika safari taratibu ikaanza ya kuondoka katika eneo hili huku mimi nikiwa katika gari moja na mkuu huyu wa hichi kikiso.

“Unaitwa nani?”

“Randy”

“Randy nani?”

Nikaa kimya kidogo kwa maana jina linalo fwatia nina tumia la mama yangu tofauti na watu wengine wanao tumia majina ya baba zao.

“Randy Yemi”

“Mhmmmm”

Alizungumza huku akitingisha kichwa chake. Hakuniongelesha kitu cha aina yoyote, tukafika kwenye moja ya eneo wezangu wote wakashushwa kwenye magari na wakaanza kufungwa vitambaa vyeusi usoni mwao. Nikatamani kuulisha ila nikashindwa kwa maana sijajua ni kwa nini nimepata nafasi ya upendeleo wa mimi kuendelea kuwepo katika gari la mkuu.

“Tumewafunga vitambaa ili wasiweze kufahamu ni wapi tunawapekea”

Mkuu huyu alizungumza huku gari magari yakikunja kona, na kuacha barabara ya lami na kuanza kuingia porini. Safari ikaendelea huku kwa muda wote akili yangu ipo makini kuhakikisha kwamba nina weza kufahamu njia tunayo pita. Safari ikatugarimu kama masaa matano jambo ambalo likisha nichosha hata katika kuikwemisha hii njia ya humu porini. Tukafika kwenye moja ya ukuta mkubwa sana wa matofali, huku kukiwa na mageti mawili makubwa sana. Magari yakaingia kwenye ngome hii, ambapo ndani kuna majengo kadhaa mazuri huku kukiwa na idadi kubwa ya wanajeshi pamoja na vifaru vya kijeshi. Kwa namna moja hii ni kambia mbayo imekamilika na jeshi lake linajimudu vizuri.

“Tumefika, sheria namba moja, ukionyesha una dalili yoyote ya kuwa msaliti ni lazima uwawe kwa kupigwa risasi adharani. Msaliti kwenye jeshi langu mimi simuhitaji.”

“Sawa sawa”

Nilizungmza huku nikimtazama mzee huyu usoni mwake. Akafunguliwa mlango na msaidizi wake, taratibu akashuka ndani ya gari na mimi nikashuka upande wangu.

“Una kitu umekichomeka kwenye mkanda wako, kisome kwa maana kila nguo uliyo kuja nayo hapa itachomwa moto”

Nikastuka sana sana na kujiuliza amekuaje mzee huyu kama kuna kitu nimekichomeka kwenye mkanda wa suruali yangu. Nikaichomoa barua hii huku mzee huyu akinitazama usoni mwangu, nikaifungua taratibu na kukuta ikiwa imeandikwa maandishi machache.

‘RANDY NINA KUPENDA, WEWE NDIO TUMAINI LANGU NJOO UNIOKOE’

“Chana”

Mzee huyo aliniamrisha huku akiwa amekaa umbali fulani ambao hata hawezi kutambua kwamba nimemaliza kusoma au laa. Nikaichana barua hii katika vipande vidogo vidogo, nikawaona wezangu wakiwavua nguo zao na kubaki uchi kabisa kama walivyo zaliwa.

“Vua nguo zako na uende ukajumuike na wezako”

“Sawa”

Nikavua nguo zangu zote na kubaki kama nilivyo zaliwa, kisha nikaelekea sehemu walipo wezangu. Akaja daktari na akaanza kumkagua mtu mmoja baada ya mwengine kwa kumtanua makalio yake.

‘Ehee ni ujinga gani tena huu?’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikiendelea kumtazama daktari huyo akimulika mulika watu katikati ya makalio na tochi ndogo yenye mwanga mkali. Kila alivyo zidi kukagua ndivyo jinsi watu walivyo gawa kwenye makundi mawili, huku kundi moja likiwa na watu wachache sana. Ikafika zangu yangu ya kukaguliwa, nikainamishwa kwa nguvu na wanajeshi wengine, daktari akanikagua kwenye makalio yangu kisha akanionyesha nikakae kwenye kundi la watu wengi. Zoezi hili likaendelea hadi kwa mtu wa mwisho na watu kama kumi na moja hivi wapo kwenye kundi lao.

Wau hao kumi na moja wakaamrisha kupanga mstari wao, mzee huyu ambaye ndio mkuu wa hili jeshi, akasimama nyuma yao huku akiwa ameshika bastola yake. Tukastuka sana baada ya kumuona akimpiga risasi ya kichwa mmoja wa vijana, vijana hao wakataka kukimbia ila wakazuiwa na wanajeshi wengine. Akaendelea kuwapiga risasi za vichwa hadi akamaliza vijana wote kumi na moja jambo lililo tufanya tuogope sana.

“Dini yetu ya kiislam, hairuhusu watu wenye asili ya ushoga kujumuika nasi kwenye vita kama hii. Hawa wote nilio waua, ni mashoga ambao huko mitaani walisha ingiliwa kimwili na wanaume wezao. Sasa endapo ukabainika kama una tabia hii, hakika tutakuua hadharani na kukutangaza kwamba wewe ni shoga. Mfiraj** na mfirwaj** wote adhabu yenu itakuwa ni moja nimeleweka”

Wote kwa pamoja tukajibu ndio.

“Ukikiuka sheria utakazo pangiwa, adhabu yako ni kifo. Hakikisha kwamba munafwata sheria na taratibu mazoezi yaanze mara moja”

Tukamrishwa kuanza kukimbia eneo hili la hii ngome ambalo ni kubwa kupindukia, tukiwa uchi kabisa. Vijana wengine kusema kweli, waliwahi kuchoka, ila viboko wanavyo pokea kutoka kwa wakufunzi wetu, vinawafanya wajikaze hivyo hivyo. Kitu ambacho kina nisaidia tu pumzi nyingi niliyo nayo ambayo ilitokana na kupenda kufanya mazoezi kwenye maisha yangu ya kawaida. Siku nzima zoezi ni hili moja la kumbilia kuizunguka ngome hii ambayo kwa haraka haraka ina weza kuchukua hata ukubwa wa jiji la Lagos, sema ubaya ni kwamba eneo hili lipo porini na limezungukwa na milima, ila limezungushiwa ukuta mkubwa sana na ulinzi ni mkali wa kutosha.

Baadhi ya vijana wezangu, nikawaona wakianguka na kupoteza fahamu. Hassna na Hussein nao ni miongoni mwa vijana hao walio poteza fahamu kutokaa na kukimbia. Kifuani mwangu nikaanza kuhisi kama kunapasuka, taratibu nikajikuta nikikaa chini na kushindwa hata kusimama. Kwa haraka nikapewa huduma ya kwanza na kuingizwa kwenye gari na kurudishwa kwenye hospitali ya kambini hapa. Nikapumzishwa kwa masaa mawili, nikaruhusiwa kutoka, nikapelekwa kwenye jengo ambalo tutaishi, nikakuta nguo zangu zikiwa kitandani kwangu. Nikiwa katika hali ya kuchoka na dibwi kubwa la mawazo, akaingia mkuu wa hili jeshi, nikataka kusimama kidogo ila nikashindwa kutokaa na misuli yangu kushindwa kabisa kukimbia.

“Usihangaike”

Alizungumza huku akinitazama, akaka kwenye kitanda kilichopo mbele yangu huku akinitazama usoni mwangu. Kwa ishara akawaomba walinzi wake kuondoka kwa maana ndani ya hili bwalo tupo mimi na yeye.

“Randy kwa nini upo huku?”

Swali la mzee huyu likanistua sana na kujikuta nikimtazama usoni mwake kwa umakini sana.

“Umemkimbia mama kwa ajili gani?”

“Uma mfahamu mama yangu?”

Nilimuuliza kwa shauku kubwa sana huku nikihitaji kufahamu amemjuaje mama yangu.

“Ndio, mama yako ni……MWANANGU”

Nikastuka sana, mapigo ya moyo yakaanza kunienda mkasi kwani kwenye kipindi chote cha maisha yangu, mama hakuwahi kunionyesha ndugu yake wa aina yoyote na kila nilipo muliza alikuwa mkali kama vile alivyo kuwa mkali nikimuuliza kuhusiana na swala zima la baba yangu.



“Mwanao…..kivipi!!?”

Niliuliza huku nikiwa nimejawa na mshangao mkubwa sana.

“Kwanza unatakiwa kunitambua jina babu yako mimi ninaitwa nani?”

“Unaitwa nani?”

“Ninaitwa Samweli, ila nilibadilisha dini na kuitwa Nasri hapo ndipo nilipo tengana na kaka yangu ambaye ndio baba halisi wa mama yako.”

“Kwa hiyo unataka kuniambia kwamba wewe ni baba mdogo kwa mama yangu?”

“Ndio. Baada ya kutengana na kaka yangu kwa kipindi kikubwa sana cha takribani miaka thelathini na tisa sasa. Mimi nilihamia kwenye nchi ya Pakistan ambapo nilijiunga na wapiganaji wa kikundi cha Al-quida, huku babu yako mkubwa akimiliki kikundi chake cha Boko haramu”

“Nilisha wahi kusikia story ya hao wapiganaji wa boko haramu, kwa hiyo unataka kuniambia kwamba, kikundi hicho kilimilikiwa na babu mkubwa?”

“Yaaa, kutokana tulitengana kutokana na maswala ya kidini na maswal pia ya mke, alinichukulia mke wangu hivyo tulijenga uadui mkubwa sana ambao hata kwenye kifo chake sikuweza kukanyaga”

Babu Nasri alizungumza kwa sauti ya upole sana huku akinitazama.

“Kwa hiyo mama yako niluonana naye akiwa katoto kadogo sana, ila bado nina endelea kumfwatilia sana kwa maana mimi ndio ndugu yake niliye baki na mimi wanangu wawili nilio wazaa nchini Pakistan na mwanamke mmoja wa kiarabu waliuwawa siku moja kwenye shambulizi lililo fanywa na majeshi ya Marekani, hivyo nilirudi hapa Niger na kutokana na msaada nilii weza kupewa na viongozi wangu wa Al-quida kipindi kile alikuwa Osama Bin Laden basi niliweza kufanikiwa kuunda kikosi changu na gome yangu hii na hadi sasa hivi nina wanajeshi zaidi ya laki nane”

“Duu, ssa babu mdogo, unataka kuniambia kwamba una mfahamu baba yangu?”

Babu Nasri akaka kimya kwa muda huku akitingisha kichwa akimaanisha kwamba ana mfahamu baba yangu.

“Anaitwa nani baba yangu?”

Niliuliza huku nikiwa na shahuku kubwa sana ya kuweza kumfahamu baba yangu hata jina lake. Simu ya babu ikaanza kuita, akaitoa kwenye koti lake la kijeshi alilo vaa na kuipokea.

“Ndio”

“Ninakuja sasa hivi”

Babu baada ya kukata simu akanyanyuka, akanitazama kwa sekunde kadhaa na kuanza kutembea kuelekea nje na hakunijibu kitu chochote, nikatamani kumfwata ili anijibu japo swali langu, ila kutokana na hali ya misuli yangu kuwa na maumivu makali sana, nikashindwa kabisa kumfwata. Kidogo matumaini ya kumfahamu baba yangu yakaanza kufufuka kwenye moyo wangu kwani tayari nimesha mpata mtu ambaye anaweza kunisaidia japo kumtafuta baba yangu.

Siku zikazidi kwenda, huku tukizidi kupata mafunzo makali ya kijeshi. Kila siku nilipo jaribu kutafuta nafasi ya kumtafuta babu yangu nilishindwa kabisa kuweza kumpata na kila mlinzi wake niliye muuliza aliweza kunieleza kwamba babu yupo kwenye dhiara za kikazi katika bala la Asia. Juhudi yangu na kupenda kwangu mazoezi, kukanipa nafasi nzuri ya kupendwa na waalimu wangu wa mazoezi na hata wezangu wengine, kwani kila mazoezi niliyafanya kwa moyo mmoja huku akilini mwangu sauti ya mama akinihitaji niweze kuwa jasiri kama baba yangu ikiendelea kujirudia rudia kadri ya siku zinavyo kwenda. Leo ni siku ya saba toka tuingie katika ngome hii, akilini mwangu bado nina mkumbuka Farida aliye niomba niweze kumsaidia na nilimuahidi kwama nitamsaidia baada ya wiki moja tu. Mawazo haya yakanifanya nizidi kuchanganyikiwa kwani hadi leo sijapata hata mbinu ya kuweza kutoroka.

“Randy mwalimu wa maoezi ana kuita”

Hussein aliniambia huku akiwa amesimama pembeni ya kitanda changu. Taratibu nikanyanyuka, nikachukua koti langu la sare ya jeshi hili, nikaanza kutembea kwa haraka kuelekea nje. Nikamkuta mwalimu wangu ambaye ni rafiki yangu sana.

“Umelala?”

“Bado mkuu”

“Sasa leo nahitaji twende mjini kidogo ukatembeze tembeze macho?”

“Mzee akifahamu itakuwaje?”

“Ni pendekezo kutoka kwake kwa maanani nilikuwa nikimuelezea kuhusiana na sifa zako juu ya mazoezi yako, akaniomba leo niweze kukutembeza mjini”

Moyo wangu ukaanza kujawa na furaha sana kwani ni nafasi yangu ya pekee ambayo ninaweza kwenda kumukoa Farida.

“Hapa kambini hayupo, ila nilizungumza naye kupitia video call”

“Sawa sawa, hata hivi nilivyo vaa si sawa tu?”

“Yaa hakuna tatizo”

Tukaelekea eneo la maegesho ya magari, tukapanda kwenye gari aina ya Jeep ambayo ni ndogo tu, na ina uwezo wa kuingia watu wawili, dereva na abiria mmoja. Tukatoka katika ngome hii na safari ikaanza. Moyoni mwangu nikaanza kufikiria ni mipango gani ambayo ninaweza kuipanga ya kuingia katika nyumba ya mzee Khalid na kuondoka na mke wake pasipo yeye mwenyewe kufahamu.

“Mwalimu”

“Ndio”

“Kuna jambo moja ninaomba nikushirikishe”

“Jambo gani?”

“Kuna mwanamme mmoja nina hitaji kumtorosha leo kwa mume wake”

“Leo hii?”

“Ndio”

“Ni nani kwako?”

“Ni….ni….?”

“Mpenzi wako?”

“Ndio”

Ilibidi kuongopea japo mimi na Farida bado hatujalizungumzia swala zima la mahusiano yetu.

“Ila umesema ni mke wa mtu, huoni kwamba inaweza kukuletea tabu hapo baadae?”

“Ni mwanaume mwenye wake wawili, na huyo mdogo ndio mpenzi wangu, ila ana mtesa na ni mtoto mdogo sana”

“Anaishi wapi?”

“Kule mjini nilipo kuwa nina ishi?”

Mwalimu akaitazama saa yake ya mkononi.

“Tukifika nitakupa dakika tano kuhakikisha kwamba unakwenda kufanya tukio hilo kimya kimya pasopo madhara ya aina yoyote, na unaondoka na huyo mwanamke yeye peke yake pasipo mtu yoyote kufahamu, kwa maana endapo ikifahamika mwanajeshi wetu ndio amefanya tukio kama hilo, basi utakwenda kuzalisha uhasama mkubwa kati ya jeshi letu na wananchi umenielewa Randy”

“Nimekuelewa mwalimu, ila kuna jambo hapo moja nahitaji kukueleza?”

“Jambo gani?”

“Ana watoto wawili mapacha?”

“Achana na swala la watoto, utakwenda kuwaweka wapi hao watoto, ikitegemea si watoto wako sawa”

Mwalimu alizugumza kwa ukali kidogo, akachomoa bastola yake moja kiunoni na kunikabidhi, nikaitoa magazine na kukuta ikiwa na risasi za kutosha, akanikabidhi na kiwambo cha kuzuia sauti, nikakifunga taratibu kwenye bastola hii.

“Kama nilivyo kueleza, hakikisha kwamba unaondoka na mwanamke na si kuondoka na mtu mwengine zaidi yake yeye”

“Sawa mwalimu”

“Na jambo hili libaki siri kati yangu mimi na wewe sawa”

“Sawa”

Tukafika katika mji ambao tunaishi, tukaingia kwenye moja ya baa ambayo kuna wanawake wengi wanao jiuza. Hapa ndipo nikagundua udhaifu wa mwalimu wangu upo kwa wanawake kwani kitendo cha kuingia ndani ya baa hii akaanza kuwashika shika wanawake hawa makalio.

“Hei Randy una dakika tano za kwenda kufanya unalo taka kulifanya, baada ya hapo rudi hapa na mwanamke huyo”

“Sawa mwalimu”

Nikataka kuondoka, ila akanishika mkono na tukasogea pembeni kidogo.

“Haya mavazi yako nisinge penda kuyatumie kwenye kazi yako?”

“Nitapata wapi mavazi mengine?”

“Wewe ni mwana jeshi, jiongeze”

Mwalimu baada ya kualiza kuzungumza maneno hayo, akawachukua wanawake wawili ambao tayari alisha wakagua kwa kuwashika shika makalio na akaondoka nao. Nikashusha pumzi huku macho yangu yakianza kufanya kazi ya kutazama ni mwanaume gani ambaye ninaweza kuyatumia mavazi yake. Nikamuona jamaa mmoja akielekea chooni huku akiwa amevalia tisheti yeusi, suruali yeusi na koti kubwa linalo fika magotini huku nalo likiwa na rangi nyeusi.

“Huyu huyu”

Nilizungungumza huku nikianza kumfwata kueleka chooni. Tukaingia choni sote wawili, akasimama katika sehemu ya kukojolea na kanza kukojoa taratibu, huku akiyumba nyumba. Nikakagua chooni humu kwa haraka na nikagundua kwamba tupo sisi wawili, nikamfwata kwa nyuma na kumpiga kabari ambayo, hakumaliza hata dakika mbili, akapoteza fahamu. Nikamvua nguo zake zote, kisha nami nikavua nguo zangu zote, na nikazivaa za kwake. Nikaichomeka bastola yangu iunoni kisha nguo zangu za jeshi nikazikunja vizuri na nikatoka chooni humu na hakuna mtu ambaye aliweza kufahamu ni kitu gani kilicho tokea, choni. Nikiwa katika kukatiza katiza kueleka nje, nikamuona jaa mmoja amning’iniza kitambaa cheusi katika mfuko wa nyuma wa suruali yake, nikakichomoa kitambaa hicho pasipo yeye mwenyewe kujua na nikaeleka nje. Nikaziingiza nguo zangu za jeshi kwenye gari tulilo kuja nalo, nikawasha gari na nikaanza kuelekea kwenye mtaa ambao nilikuwa nina ishi. Nikasimamisha gari katika mtaa wa pili, kisha nikajifunga kitambaa changu usoni, na kuificha sura yangu, kwa kufaa huku ni ngumu sana mtu kuweza kunifahamu kama ni mimi. Nikazima gari, kisha nikashuka, nikatazama namba za gari hili la jeshi, nikazifungua platenumber zote na kuziweka ndani ya gari, ili kuepusha gari letu kujulikana na watu wa kawaida.

Nikakatiza katika katika mtaa huu wenye nyumba zisizo na umeme, nikika hadi nyumbani kwa mzee Khalid, nikatazama mazingira ya eneo la nyumba hii kusema kweli yametulia na sisikii mishe mishe zozote zinazo endelea, hata taa za chemli wanazo ziwasha kwa leo sizioni. Ila kutokana muda umwekwenda, nikajipa moja na kujiaminisha kwamba watakuwa wamelala.

Nikanyata hadi kwenye nyumba kubwa, nikazunguka upande lilipo dirisha la Farida, nikachungulia ndani kidogo na kuona watoto wake wakiwa wamelala kitandani huku yeye mwenyewe akiwa hayupo.

‘Fuc** yupo wapi huyu mwanamke?’

Nilizungumz akimoyo moyo huku nikinyata hadi kwenye dirisha la mzee Khalid, nikachungulia kwa umakini na nikamkuta mzee Khalifan akifanya mapenzi na mke wake mkubwa. Akili yangu kwa haraka ikanituma niende kwenye chumba changu, ila kabla sijapiga hatua, mlio wa simu ulio tokea kwenye koti hili uka nistua mimi, mzee Khalifan na mke wake ndani.

“Ni nani unaye chungulia dirishani?”

Mzee Khalifan alizungumza huku akitazama dirishani, kwa haraka nikaitoa simu hii na kuizima kabisa, nikazunguka upade wa pili wa nyumba hii. Nikakutana na Farida akitoka chumbani kwangu, alipo niona akapiga yowe moja, ila nikamuwahi mdoni mwake na kumziba kwa nguvu. Mzee Khalid, akatoka akiwa ameshika tochi kubwa pamoja na panga.

“Muachie mke wangu”

Alizungumza kwa ukali huku akimulika katika eneo tulilopo, kwa haraka nikachomoa bastola yangu na kumpiga risasi ya mguuni na kumfanya anguke chini huku akitoa kilio kikubwa. Mke wake mkubwa akatoka nje huku akipiga ukunga. Nikajikuta mkono wangu wa kulia ukielekeza bastola kichwani mwake, na kidole changu hakikufanya kosa katika kuminya triga, nikamshuhudia mama huyu akianguka chini na kutulia kimya. Farida akaendela kujaribu kujitoa mikononi mwangu huku akijaribu kuomba msaada.

“Ni mimi”

Nilimnong’oneza kwa nguvu. Nikaanza kusikia majirani wakiaka kutoa kwenye nyumba zao huku wakipiga filimbi za kuamshana wakiashiria kwamba kuna uvamizi umetokea. Nikamuchia Farida, nikampiga teke la shigo mzee Khalid, na akapoteza fahamu. Nikamshika Farida mkono na kuanza kukimbia naye huku tukijaribu kuhakikisha kwamba tunawatoka raia wanao elekea kwenye nyumba ya mzee Khalid.

“Huku”

Farida alizungumza huku tukikatiza kwenye vichochoro ambavyo sio rahisi kwa watu kufahamu kama tunapita huku. Kwa bahati vichochoro tulivyo pita, tulitokea katika mtaa ambao nimeliacha gari nililo kuja nalo.

“Nisubiri hapa”

Nilizungumza na Farida akajibanza kwenye moja ya kichochoro, nikakimbilia hadi gari lilipo. Nikapanda kwenye gari kwa umakini, nikaliwasha na kuligeuza kwa kasi sana na kuelekea hadi kichochoro kilipo, Farida akaingia ndani ya gari na tukaondoka eneo hili huku nikivua kivua kitambaa changu usoni.

“Randy wanangu tumewaacha?”

Farida alizungumza huku akitazama nyuma.

“Hatuwezi kurudi huko”

Nilizungumza huku nikiongeza mwendo kasi wa gari langu. Kwa usalama sikuhitaji kuelekea katika baa ambayo tumefikizia na mwalimu wangu.

“Tunakwenda wapi?”

Farida alizungumza huku akivua kitambaa kilicho funika uso wake.

“Nahitaji kufanya jambo”

“Jambo gani?”

“Nahitaji usiku huu huu utoke katika nchi hii na kwenda Nigeria”

“Nitoke mimi peka yangu na wewe je?”

“Mimi nitarudi kambini”

“Randt, siwezi bwana”

“Huwezi nini?”

“Nataka nibaki na wewe?”

Taratibu nikapunguza mwendo kasi wa gari hili na kulisimamisha pembezoni mwa barabara.

“Farida, kumbuka hapa nimetoroka jeshini, sina uwezo wa kukupeleka sehemu nyingine tofauti na Nigeria, sina nyumba na sina chochote, kitu ambacho ninaweza kukusaidia kwa sasa ni kukufikisha mpakani ambapo nitakupa maelekezo ya wapi uende”

“Randy sitaki kusikia hilo nakupenda, nakuhitaji Randy”

Farida alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake. Nikashusha pumzi nyingi huku nikitafakari ni nini cha kufanya. Nikaanza kuvua nguo nilizo zivaa, kisha nikavaa nguo za jeshi.

“Unaenda wapi Randy”

Farida aliniluliza mara baada ya kuniona ninashuka kwenye gari, sikumjibu kitu chochote zaidi ya kuzifunga namba za gari hili mbele na nyuma, kisha nguo hizo nikazichukua na kuingia nazo kwenye kichaka, nikaitoa simu ambayo ipo ndani ya koti hili, nikakuta na pesa kiasi. Nikaziweka sehemu moja kisha nikarudi kwenye gari na kumkuta Farida akiendeleak ulia, nikachukua kidungu cha mafuta ya petrol pamoja na kiberiti, nikarudi katika sehemu nilipo acha nguo nilizo fanyia tukio, nikazimwagia mafuta ya kutosha kisha nika zichoma moto, ndani ya muda mchache zikawa zimeteketea zote. Nikarudi kwenye gari, nikakiweka kidungu cha mafuta sehemu nilipo kitoa.

“Turudi”

Nilizungumza huku nikiwasha gari”

“Wapi?”

“Tunaelekea mjini”

“Randy huoni ni hatari?”

“Tuho shuka kwenye gari, kwani ndani ya baibui lako umavaa nini?”

“Sidiria na skintait”

“Poa”

Nikawasga gari na kugeuza, tukarudi hadi kwenye baa ambayo nilimuacha mwalimu.

“Hakikisha kwamba hushuki kwenye gari, na laza siti yako usionekane na watu wa nje sawa”

“Sawa”

“Funga milango kwa ndani”

“Sawa”

Nikashuka kwenye gari na kuelekea katika chumba ambacho mwalimu aliingia na malaya wake. Mapigoa ya moyo yakaanza kunienda mbio sana, mara baada ya kumkuta mwalimu akiwa amechomwa visu vya vifuani na kufia katika sofa aliko kalia huku uume wake ukiwa umekatwa na malaya alio ingia nao ndani ya chumba hichi wote wawili hawapo jambo lililo nifanya nichomoe bastola yangu huku wasiwasi mwingi sana na woga ukinitawala kwenye mwili wangu.



Nikatoka chumbani humu huku nikiwa makini sana, macho yangu yakaanza kuangaza kila sehemu katika baa hii, kila mtu ana endelea na shuhuli zake kama hakuna jambo lolote lililo tokea. Nikairudisha bastola yagu kiunoni mwangu. Nikarudi ndani ya gari huku nikiwa nimachanganyikiwa sana hali iliyo mfanya hadi farida na yeye kuweza kuligundua hilo.

“Vipi kuna nini?”

“Mmmmm……”

“Randy niambie kuna nini kilicho tokea ndani humu?”

“Tuondoke hili eneo sio salama”

Nilizungumza huku nikiwasha gari, tukaondoka eneo hili kwa kasi kubwa sana hadi Farida akanishia mkono wangu wa kulia.

“Punguza mwendo Randy”

Sikuhitaji kumsikiza Farida zaidi ya kuhiyaji kufwata kile kinacho endelea kichwani mwangu. Safari ikazidi kupamba moto, nikaitoa simu niliyo ikuta kwenye koti la mtu ambaye nilimpokonya nguo zake. Nikaiwasha huku nikipunguza mwendo kasi wa gari hili. Mtu ambaye kwa sasa nina weza kumuomba msaada na akanielewa ni mzee Uchuku, meneja wa mama katika mambo mengi sana. Ni mwanaume msikivu na aliye ishika dini yake vizuri na ana roho ya huruma sana. Nikaingiza namba zake za simu, kisha nikampigia, simu yake ikaanza kuita na baada ya muda ikapokelewa.

“Haloo mzee”

“Hei Randy”

“Ndio mzee wangu, nina kuomba usimuambie mama chochote ambacho ambacho ninahitaji kuzungumza na wewe”

“Sawa zungumza, nipo kwangu kwanza na mbona umenipigia na namba ya Niger ndio sehemu ulipo?”

“Ndio, ila nina shida mzee”

“Shida gani?”

“Ninahitaji msaada wa kuondoka kwenye hii haraka iwezekanavyo kuna watu wana hitaji kuniua”

“Kuku ua, kwa nini usirudi nchini Nigeria na ukaendelea na maisha?”

“Mzee wangu huko ndipo matatizo yangu yalipo anzia, nilisha pigwa risasi moja ya kifuani na nimefanya kuotokwa huku Niger”

“Hili ni swala muhimu Randy, lazima mama yako aweze kufahamu na ni nani ambye alikupiga risasi?”

“Mzee wangu ninakuomba niweze kupata msaada wako, hayo mambo mengine hatuwezi kuzungumza kwenye simu”

“Ohoo Mungu wangu”

“Na ninakuomba usimuambie mama chochote juu ya hili”

“Sasa nenda kwenye hoteli ya mama yako, tumua code yangu ya 1269K sawa, ninawapigia waweze kukuwekea chumba”

“Nashukuru sana, ila nina kuomba usimuambie mama kuhusiana na kitu cha aina yoyote mama.”

“Sinto muambiaba nina mambo mengi ambayo kesho nitakuja huku tuweze kuzungumza kwa pamoja”

“Sawa, ila mama yangu ana endeleaje?”

“Yupo vizuri, anaendelea na utendaji wake wa kazi kama kawaida?”

“Haja nimiss?”

“Nisiwe mnafki katika hilo, sijawahi kumsikia akikuzungumzika, toka siku ile ulivyo ondoka kwa aibu ofisini kwake”

“Sawa, ila hii simu sio yangu, na usitumie kabisa, utanikuta hotelini”

“Sawa sawa”

Nikakata simu hii na kuirusha pembezoni mwa barabara.

“Ulikuwa una zungumza na nani?”

Farida alizungumza huku akinitazama usoni mwangu

“Utamuona kesho akija”

Nilizungumza huku nikibadilisha njia na kuelekea katika mji ambao ipo hoteli yetu moja kubwa ya kitalii, ila ina meneja wake ambaye ana isimamia kwa niaba ya mama. Ikatugarimu kama masaa matu na nusu kufika katika hoteli hii, tukashuka kwenye gari namoja kwa moja tukaelekea mapokezi jambo lililo fanyanya hata wahudumu kushangaa, mavazi niliyo yavaa, kwani nahisi walivyo ambiwa kwamba nitakuja hapa, wakahisi nitakuwa nimevalia suti nzuri. Nikawatajia code maalumu ambayo meneja wa mama huwa ana itumia kwenye hoteli zote barani Afrika zinazo milikiwa na mama yangu.

“Wewe kweli ni Randy Yemi”

“Aisee mbona una maswali mengi, unahisi hizo code mimi nitaziota namba kadi bwana”

Nilimjibu kwa ukali dada huyu wa mapokezi, akanikabidhi kadi, nikamshika Farida mkono na kuingianaye kwenye lifti. Tukaelekea hadi kwenye gorofa ya ishirini na tano ambayo ndio ya mwisho. Tukaanza kutembea kwenye kordo hii ndefu huku Farida akionekana kujawa na mshangao wa kila anacho kiona. Nilipo fika katika mlango wa chumba tunacho takiwa kingia, nikaipitisha kadi niliyo pewa kwenye kitasa maalumu kinacho tumia umeme, na kikanihitaji kuingiza code nilizo tajiwa na meneja wa mama. Nikaziandika kwa haraka na mlango ukafungua. Nikachomoa bastola yangu na kuanza kukagua sehemu moja baada ya nyingie huku nikiwa makini sana, nilipo hakikisha kwamba kuna usalama wa kutosha, nikazima taa zenye mwanga mkal na kubakisha taa zenye mwanga mdogo kiasi.

“Pole”

Farida alizungumza huku akikaa kitandani, nikamtazama kwa sekunde kadhaa, kisha nikamfwata kitandani alipo keti, nikashika shavu la upande wake wa kushoto.

“Maisha yangu nimeyatoa kwa ajili yako Farida, hichi nilicho kifanya ni kitu hatari sana na kinaweza kunifanya maisha yangu yawe ya tabu sana hapo baade”

Nilizungumza kwa upole na unyonge huku nikiendelea kumtazama Farida usoni mwake.

“Usijali Randy mwenyezi Mungu atakuwa pamoja nasi”

“Amen, ila nahisi maisha yangu hayato kuwa na amani, yatakuwa ni maisha ya kuhangaika tu”

“Randy ukizungumza hivyo na shetani naye ana tilia mkazo kwenye hili mpenzi wangu. Ninakuomba uwe na amani sawa mpenzi wangu”

Farida alizungumza kwa sauti ya upole, akaanza kuvua baibui lake hili zito alilo livaa, hapa ndipo nikapata wasaa wa kuufaidi mwili wake vizuri.

‘Kum***e huyu mzee alikuwa ana faidi’

Nilijisemea kimoyo moyo huku nikitazama hispi nene na kalio la maana alilo jaliwa Farida. Sikuwahitaji maongezi ya aina yoyote kwa maana muda wenyewe ni mchache na sifahamu matatizo yanaweza kutokea muda gani. Nikamvuta Farida na kuanza kumnyonya midomo yake kwa kasi ya ajabu huku viganja vyangu vikiendelea kushereke jinsi inavyo tomasa mwili wa mwanamke huyo.

Farida akaanza kufungua vifungo vya shati langu hili la jeshi nililo livaa, kwa haraka nikalivua shati hili, akaanza kukilamba kifua changu taratibu, mihemo ya Farida, ikazidi kunisisimua na kunifanya nizidi kuchanganyikiwa kwani nina muda mrefu kwa kweli sijawahi kupama penzi la mwanamke.

Farida akafungua mkanda wangu sa suruali, akahamia kweye kifungo cha suali na mwishowe akaingia mkono kwenye boksa nilivyo ivaa na kumchomoa jogoo wangu aliye nono vizuri. Farida kama simba jike mwenye njaa, akamdumbukiza jogoo wangu mdomoni mwake na kuanza kumfanyia fujo ya za kumnyonya hadi mimimwenye nikazidi kuchanganyikiwa. Nikamvua Farida sidiria yake na kuanza kuyatomasa maziwa yake. Tukaanza kupeana burudani ambayo kusema kweli, niliikamia kwa kipindi kirefu, shida zangu juu ya matatizo yaliyo tokea kwenye familia ya mzee Khalid pamoja na mwalimu wangu wa jeshi, zote nikazisahau. Kwa jinsi ninavyo jiamini katika kutawala kila mchezo ninao kutana na kila mwanamke, ila kwa Farida ni tofauti kwa maana kila ninavyo mpeleka anahimili mikiki mikiki yangu. Farida akanilaza chini kisha akaanza kumkalia jogoo wangu na kuanza kuzungusha kiuno chake, hakika wanawake wa kiafrika wamebarikiwa, hususani Farida. Hadi tuna maliza mzunguko wa kwanza, mwenzangu anaonekana ana uhitaji wa penzi langu jamabo ambalo sikuwahi kukutana nalo kwa mwanamke wa ina yoyote toka nifahamu maswala juu ya mahusiano.

“Farida mbona muonekano wako hauonyeshi kama haya mambo huyafahamu?”

“Toka kuzaliwa kwangu sijawahu kuridhishwa na mwanaume zaidi ya leo?”

“Una uhakika na unacho kizungumza?”

“Haki ya Mungu, Randy siwezi kukutania. Mimi raha ya mwanaume sijawahi kuipata zaidi ya kwako, ndio maana unaniona nina furaha na hapa bado nina hitaji kuendelea na penzi lako”

“Kweli?”

“Kweli Randy, yule mzee alitaka kunizeesha na nyege zangu tu”

Tukio la kumuua mke wa mzee Khalid likajirudia kichwani mwangu na kujikuta nikipoteza furaha kabisa.

“Baby mbona umepoteza furaha?”

“Uliweza kuhushudia tukio la mke mwenzio?”

“Ndio”

“Linaninyima furaha kwa kweli”

“Usijali mume wangu, nitakutunzia siri hii hadi mwisho wa uhai wangu?”

“Unauhakika na unacho kizungumza?”

“Haki ya Mungu, nakuahidi hilo Randy, nitakutunzia siri na nipo tayari kufa kwa ajili yako”

“Kwa nini umenipenda?”

“Nilikupenda toka siku ya kwanza unaletwa nyumbani pale, na sikuhitaji uzitambue hisia zangu ndio maana siku zote nilikuwa nina jificha sura yangu ili usije ukaniona na kunitamani”

Farida alizungumza kwa sauti ya upole huku akinitazama usoni mwangu.

“Randy nimeamua kuachana na kila kitu kwa ajili yako, ninakupenda sana mpenzi wangu”

Farida akaushusha mkono wake wa kulia hadi kwenye jogoo wangu, akaanza kumshika taratibu hazikupita hata dakika mbili jogoo wangu akasimama wima, taratibu Farida akamkalia na shuhuli ikaendelea. Mzunguko huu wa pili ukawa ni wa kukata na shoka. Baada ya mtanange huu, usingizi mzito ukatupitia na tuka lala fofofo.

Kengele ya mlangoni ikanistua na nikakurupuka kitandani, nikamtazama Farida na nikamkuta akiwa amelala, kwa jinsi umbo lake lilivyo hakika, nikajikuta nikizidi kumtamani. Nikautazama mlango huu, nikamfunika Farida na shuka zito nusu ya mwili wake, kisha nikachukua suruali yangu na kuivaa, nikaishika bastola yangu, nikatembea hadi mlangoni, nikafungua kwa kutumia kadi hii, nikakutana na sura ya mzee Uchuku, nikachungulia na nikamkuta yupo peke yake.

“Karibu”

Nilizungumza huku bastola yangu nikiichomeka kiunoni. Mzee Uchuku akaingia, akashangaa kumuona Farida kitanda, ila nikamkaribisha kwenye seble ndogo iliyomo ndani ya chumba hichi. Nikamsalimia kwa heshima mzee huyu kwa maana kwa sasa yeye ndio msaada kwangu.

“Umekuwa mwanajeshi?”

“Ndio, ila sihitaji kuendelea kuwa katika jeshi hilo tena”

“Ni jeshi gani?”

“Kwa sasa sihitaji kulizungumzia hilo, nina hitaji hivi sasa uweze kunisaidia kutoka katika nchi hii ya Niger naamii kuna mambo mabaya yanayo weze kunitokea.”

“Sasa mimi nimekuja na hati ya kusafiria moja, huyu mwanamke upo pamoja naye?”

“Ndio”

“Sasa itakuwaje?”

“Nisaidie kupata hati ya huyu binti, tunahitaji kwenda mbali na hapa”

“Randy sasa huu ni mtihani kwa mana imenibidi niweze kutafuta hati ambayo haina jina lako ila ina picha yako”

“Kwani hapa Niger hujuani na watu kwenye kitengo cha uahamiaji?”

“Najuana nao na ndio ambao waliweza kunisaidia na nimepitia huko kabla ya kuja hapa”

“Sawa, naomba unisaidie katika hili”

“Muamshe basi mpenzi wako, ili kama kuna uwezekano niweze kumsaidia”

“Sawa sawa”

Nikanyanyuka kwenye sofa na kumfwata Farida kitandani

“Hei unaweza kuvaa nguo na ukaja tuzungumze na meneja wa maam”

“Sawa mume wangu”

Faria akavaa baibui lake kisha tukarudi sebleni, akasalimiana na meneja.

“Huyu ni meneja wa mama yangu, huwa ndio mratibu wa kampuni zote za mama, na ndio mtu ninaye weza kumuamini kwa wakati huu.”

“Nashukuru kukufahamu”

“Mzee huyu ni Farida, ni mpenzi wangu mpya mwanamke ambaye alinisaidia nilipo pigwa risasi, akaniuguza nyumbani kwake hadi nimepona sasa.”

“Nashukuru kukufahamu na asante kwa msaada wako kwa kijana wetu”

“Nashukuru pia”

“Basi inabidi nikupige picha ili nizipelekea uhamiaji sasa hivi wakutengenezee hati yako ya kusafiria na maswala ya kusafiri tutajua nitakapo rudi”

“Sawa”

Meneja akampiga Farida picha kadhaa, kisha akanikabidhi simu yake moja ambayo ameniahidi endapo kutahitajika taarifa yoyote unayo husiana na Farida basi atanifahamisha. Tukaagana na meneja kisha akaondoka, tukaletewa kifungua kinywa na muhudumu.

“Randy”

“Naam”

“Unataka kuniambia kwamba hii hoteli yote ni hoteli ya mama yako?”

“Ndio”

“Sasa kwa nini usiwe unafanya kazi kwenye japo moja ya kampuni ya mama yako, kuliko kuishi maisha ya kukimbizana kimbizana hivi?”

“Mama yangu hanipendi”

“Kwa nini?”

“Sijaijua kwa kweli sababu yake ya msingi ya kuto kunipenda, ila hana mapenzi na mimi. Isitoshe mimi ndio mtoto wake wa pekee na hana mtoto mwengine zaidi yangu”

“Masikiniii pole”

“Asante ndio maana umeona niliamua kuishi huku huku Niger, ili mradi moyo wangu uweze kupata amani. Ila hapa pia pamenishinda. Ninajaribu kumtafuta baba yangu ili niweze kufahamu uhalisia wangu mimi upo wapi, ila ina shindwa kumpata mtu ambaye anaweza kuniambia ukweli juu ya baba yangu”

Kabla sijazungumza kitu chochote, simu aliyo niachia meneja ikaanza kuita, nikaitazama kwa muda, kutokana alinihakikishia kwmaba yeye ndio mtu wa pekee ambaye anaweza kupiga katika simu hiyo sikuwa n awasiwasi zaidi ya kuipokea.

“Randy”

Niliisikia sauti ya meneja akiniita huku akionekana kujawa na mashaka.

“Ndio meneja”

“Kama upo karibu na huyo mwanamke nakuomba uingie bafuni nina mazungumzo muhimu sana na wewe na hutakiwi kuweza kuyafahamu mazungumzo hayo.”

Nikamtazama Farida huku nikiwa ninatabasamu, nikachomoa bastola yangu na kuiweka mezani,kisha nikanyanyuka na kuingia bafuni na nikaufunga mlango kwa ndani.

“Sawa zungumza mzee”

“Ninakuomba ufanye unacho weza kukifahanya ila naomba umtoroke huyo mwanamke wako uliye naye si mtu mzuri kabisa Randy”

“Kwa nini?”

“Mwanamke huyo ni Gaidi wa kike na anafanya kazi chini ya kundi la kigaidi la Al-quida na ninavyo zungumza hivi sasa wana usalama wapo njiani wanakuja hapo hotelini kumkamata nimebanwa nanimeshindwa kuficha siri na niliamua kueleza ukweli wa wapi alipo mwanamke huyo”

Mwili mzima ukaanza kunitetemeka, kwani hii habari ninayo ambiwa ni mpya kabisa, habari ambayo kwenye ufahamu wa akili zangu wala sikuweza kutarajia kama Farida ni gaidi tena wa kundi la Al-quida



Hata kabla sijamaliza kukata simu nikaanza kusikia vishindo sebleni ambavyo kwa haraka vikanifanya nifungue mlango huu wa bafuni huku simu nikiwa nimeishika mkononi. Nikamshuhudia Farida akipambana na askari wa kikosi maalumu cha serikali, ambao naamini ndio hao ambao meneja amenieleza kwamba wanakuja kumkamta Farida. Mapigo ambayo Farida anawapiga wana usalama hao kusema kweli yakaniweka katika hali ya mshangao sana, na kila mwana usalama aliye pigwa, hakunyanyuka na wengine waliishia kuuwawa. Ndani ya dakika tano nilizo shuhudia mapigano haya, wana usalama wote kumi na moja walio agizwa kuja katika eneo hili wamepigwa na kutulia chini”

“Tubadilishe nguo haraka haraka na tutoke eneo hili”

Farida alizungumza huku akiwapiga risasi za vichwa kwa kutumia bastola yangu niliyo ifunga kiwambo cha kuzuia sauti. Farida alipo hakikisha kwamba zoezi lake limekamilika akachungulia nje ya mlango kisha akafunga mlango huu kwa ndani. Tukaanza kuwavua wanajeshi hawa nguo huku mwili mzima ukiwa umeishiwa hata hamu ya kuwa na mwanamke huyu.

“Wewe ni nani?”

Nilimuuliza huku nikiwa nimejawa na sauti iliyo jaa utetemesho mkubwa sana.

“Vaa nguo, huu si muda wa kuulizana maswali”

Farida alizungumza kwa kujiamini na kwa sauti ambayo dhairi inamuonyesha yeye si mtu wa mchezo mchezo. Nikavua suruali yangu na kuvaa nguo za moja ya wana usalama hawa, ambao uzuri ni kwamba mavazi waliyo yavaa, yameambatana na kofia za chuma pamoja na kofia ambazo zote zimetawanyishwa na kila kofia imeangukia upande wake. Tulipo hakikisha kwamba tumevaa kama wana usalama hawa, Farida akanikabidhi bunduki pamoja na bastola mbili.

“Tunatakiwa kutoka humu ndani tukiwa salama sawa?”

“Sawa”

Farida akakimbilia dirishani na kuchungulia, kisha akarudi nilipo simama, nikataka kuichukua simu niliyo iweka mezani ila akanikataza, akaipiga simu hiyo na ikatawanyika vipande vipande. Tukatoka nje na kuanza kutembea kwenye kordo hii kwa kujiamini sana huku macho yangu kila ninavyo jaribu kumtafakari mwanamke huyu ambaye aliniomba msaada wa kumuondoa katika familia ya mzee Khalid, ninashindwa kumpatia majibu ya kueleweka kwa kweli. Tukafika kwenye lifti hizi mbili, tukaona zote zina pandisha juu.

“Simama pembeni”

Farida alizungumza huku akichomoa mabomu mawili ya kurusha kwa mkono, kitendo cha lifti kufunguka akayatutupia mabomu hayo mawili ndani ya lifti hizi zilizo jaa wana usalama. Milipuko mikubwa ikaambatana na vilio vya maumivu vya wana usalama hao huku kengele ya hatari ya gofa hii ikianza kulia na vibomba maalumu vya kumwaga maji pale kunapo tokea ajali ya moto, vikaanza kufanya kazi ya kumwaga maji.

“Tutumie ngazi kushuka chini”

“Sawa”

Tukaanza kushuka kwenye ngazi huku wateja wa kila gorofa wakitoka na mataulo yao kuokoa maisha yao kwani kengele hii inaashiria jengo lipo katika hatari kubwa. Tukafanikiwa kufika chini kabisa, tukakuta gari za wana usalama hawa zikiwa zimezunguka katika eneo la hoteli hii. Tukajumuika katikati ya wananchi hawa wanao okoa maisha yao.

“Huku”

Farida alizungumza huku tukilifwata moja ya gari jeusi aina ya GMC TERRAIN. Farida akapanda upande wa dereva, huku nami nikipanda upande wa pili, akawasha gari hili, akalirudisha nyuma kwa kasi na kuliweka sawa na tukaondoka katika eneo hili la hotelini huku tukiwa salama salmin.

“Shitiii”

Farida alizungumza huku machozi yakimlenga lenga usoni mwake. Nikatazama nyuma ila sikuweza kuona gari ya aina yoyote ambayo itatufwatilia.

“Farida nahitaji kuweza kufahamu wewe ni nani?”

Niliuliza kwa msisitizo huku nikimtazama usoni mwake, akanitazama kwa sekunde kadhaa na kuendelea na safari hii, huku gari hili akiliendesha kwa kasi ya ajabu sana. Sikua na budi zaidi ya kunyooshea bastola ya kichwa, Farida akanitazama huku akitabasamu.

“Unataka kuniua?”

“Ikiwezekana ndio, wewe ni nani?”

Nilizungumza kwa ukali sana huku nikiendelea kumtazama. Farida akakunja kona moja kali na kunifanya niyumbe kidogo ila bastola yangu sikuweza kuiachia, tukaanza kuelekea kwenye barabara moja ya vumbi.

“Sasa hivi sio salama kulizungumzia hili mpenzi wangu naomba uwe mvumilivu?”

“Mvumilivu wa nini Farida, sikuelewi mbona, nahitaji kukufahamu wewe ni nani na kwa nini upon a mimi, kwa maana kuwa nami lazima uwe na sababu maalumu”

Niliendelea kuzungumza kwa ukali, tulipo fika kwenye moja yamsitu Farida akafunga breki za gari hili, akatoa simu ya upepo akaanza kukirokocha.

“Unanidharau?”

“Randy kwa nini hutaki kunielewa. Ninafanya haya yote kwa ajili yako, unahisi kwamba mimi ni mjinga au unahisi kwamba sikupendi eheee?”

Farida alizungumza kwa ukali sana huku akinitazama usoni mwangu.

“Nimekuambia kwamba kaa kimya nifanye kazi yangu nikimaliza nitakuambia mimi ni nani, sasa mambo kunishikia bastola ni ya nini, laiti kama ningekuwa ni mtu mbaya kwako ningekuwa nimesha kuua”

Maneno ya Farida yakanifanya taratibu nishushe pumzi nyingi huku bastola yangu nikiishusha chini.

“Zero, one, one, two. Over”

Farida alizungumza huku akiendelea kuikorokocha simu hii ya upepo.

“Zero, one, one, two Over”

“Nimekupata mkuu Over”

“Nipo kwenye eneo maalumu, Over”

“Ndani ya dakika mbili nitakuwa nimefika hapo. Over”

“Nimekuelewa. Over”

Farida mara baada ya kumaliza kuzungumza maneno hayo akaiweka simu hiyo pembeni na kunigeukia.

“Hutakiwi kunichukia mimi na unatakiwa kunishukuru mimi”

“Farida, unaniweka njia panda mpenzi wangu”

“Natambu hilo Randy, ila nilihitaji kukueleza hili swala mapema, ila nilikosa nafasi na nikajua kwamba huwezi kuniami, moja kwa uzuri wangu pili kwa kuwa tayari mwanzo nilisha jitambulisha kama mwanamke mnyonge na ninaye nyanywaswa kwenye ndoa yangu”

Tukasikia mngurumo wa helicopter, Farida akawa wa kwanza kutoka ndani ya gari kisha nami nikifwatia. Faria kwa ishara akaanza kumuelekeza rubani wa helicopter hiyo. Zikashushwa kamba mbili ndefu.

“Tunapanda juu”

Farida alizungumza huku akishika kamba moja.

“Juu?”

“Ndio hapa helicopter haiwezi kutuo kutokana na hii miti na hatuna namna nyingine”

“Ohooo”

“Ndio tupande hakuan muda wa kupoteza”

Farida akaanza kupanda kamba hii, na mimi nikaanza kupanda, kutoka nilisha pitia mazoezi ya kupanda kamba katika kikosi cha jeshi kilicho kikinifundisha, haikuniwia ugumu mkubwa sana. Tukafika ndani ya helicopter hiyo na kamba hizi zikavutwa juu na wanajeshi wawili wenye asili ya kiarabu tulio wakuta humu ndani.

“Asalam alaykum”

Farida aliwasalimia wanajeshi hawa.

“Walaykum msalam mkuu, pole kwa matatizo”

“Nashukuru. Randy kutana na vijana wangu Bashiri na Kassim”

“Nashukuru kuwafahamu”

“Bashiri na Kassim, huyu anaitwa Randy ni shemeji yenu sasa”

“Tunafurahi kukufahamu shemeji”

“Hata mimi”

“Vipi mipango yote imekwenda vizuri?”

“Ndio mkuu kila kitu kipo kwenye mstari”

“Randy tunaelekea Libya sasa, tutakaa hapo siku moja kisha tutachukua ndege na kwenda Saud Arabi na baada ya hapo tutafunga safari na kuelekea Afghanistan huko ndio nyumbani kwetu”

“Sawa”

Nilijibu kwa unyonge huku nikimtazama Farida usoni mwake. Kusema kweli maisha yangu sasa yamebadilika, mipango yangu inazidi kuharibika siku hadi siku, kwani sasa ninakwenda kuishi kwenye nchi ambazo sikuwahi kuziwazia hata siku moja kwenye maisha yangu. Safari ikatuchukua masaa kadhaa angani na tukafika katika nchi ya Libya. Tukapokelewa na wanajeshi wenngine katia eneo moja ambalo limetulia, tukaingia ndani ya gari na safari ikaanza huku Farida akionekana kuheshimiwa sana na kila mwanajeshi.

“Karibu Libya mpenzi wangu”

“Nashukuru”

“Unaonekana kwamba huna furaha sana”

“Ni uchovu tu”

“Usijali tuta pumzika sawa”

“Sawa”

Tukafika kwenye moja ya jumba moja kubwa sana ambalo ulinzi wake umeimarishwa vizuri. Tukafunguliwa milango kwenye gari hili la kushuka. Farida akamsalimia mzee mmoja kwa heshima zote huku akimbusu mkono wake wa kulia, mzee huyo akaonekana kufurahi sana kwa kumuona Farida.

“Randy huyu ni mjomba wangu. Mjomba huyu ni mume wangu mtarajiwa anaitwa Randy”

Mzee huyu akanisalimia kwa ishara hapa ndipo nikagundua kwamba mzee huyu ni bubu, nikamjibu ishara zake na akatukaribisha ndani. Tukakribishwa kwenye moja ya meza kubwa ya chakula, yukanawishwa mikono na mfanyakazi mmoja wakike.

“Karibu mume wangu, jisikie huru na jisikie amani hapa ni nyumbani kwetu kabisa”

“Sawa mpenzi”

Niliendelea kujibu kwa unyonge kwa maana kusema kweli bado nipo njia panda. Tukaanza kula chakula hichi kilicho andaliwa vizuri, na baada ya kumaliza kula tukasindikizwa na mmoja wa wafanyakazi hadi kwenye chumba kimoja tulicho andaliwa. Farida akanisogela na kunishika kiunoni mwangu.

“Randy mpenzi wangu ninakuomba uweze kunisamehe kwa kila jambo ambalo linaendelea sawa”

“Farida nitakusamehe vipi ikiwa ninajionea mapicha picha ambayo sijui ni ya kichina au ya kihindi”

“Haahahaa…”

“Unacheka?”

“Unanifurahisha sana Randy badala ya kufurahi umetoka mikononi mwa maadui zako, ila una lalama bado?”

“Lazima nilalame Farida”

“Pole mume wangu, tuvue nguo, tuoge kisha nitakuelezea historia yangu ya maisha yangu kuanzia A hadi Z, sawa baba yangu”

Farida alizungumza kwa sauti ya upole na iliyo jaa mahaba mengi sana kwangu.

“Sawa”

“Mambo ndio hayo, twende mume wangu”

Farida akanishika mkono na tukaingia kwenye moja ya bafu moja kubwa sana. Taratibu akaanza kunivua nguo zangu huku akiyachezesha chezesha macho yake kama mdoli na akanifanya nicheke.

“Acha vituko”

“Nisipo kufanyia mimi vituko ni nani atakufanyia mume wangu”

Farida alipo maliza kunivua nguo zangu, nikamvua na yeye nguo zake. Farida akaanza uchokozi wa kumshika jogoo wangu na kuanza kumchua chua huku akinitazama usoni mwangu, jogoo wangu hakulema masiraha yoyote zaidi ya kusimama. Farida taratibu akageuka na kuushika ukuta huku akinama kidogo, taratibu nikaanza kula kitumbua chake, mtanange wetu hadi unafikia tamati ukachukua nusu saa. Tukaoga na kurudi chumbani, tukajitupa kitandani huku tukiwa na maji yetu mwilini.

“Huoni kama tuna totesha kitanda?”

“Usijali kila kitu kinaweza kubadilishwa ndani ya chumba hichi”

“Duu!!”

“Yaa mjomba wangu kwenye swala la kiuchumi yupo vizuri”

“Ehee nahitaji kukujua Farida na ninakuomba usinifiche kitu chochote kwa maana ukinificha na siku nikija kugundua ukweli hakika nitakuchukia na nitakuona wewe ni muongo”

“Kwa sasa siwezi kukuficha Randy chochote kwa maana wewe ni mume wangu na wewe ndio mwanaume ambaye nilikuwa nina kuhitaji kwenye maisha yangu”

“Okay niambie”

“Kwa jina langu halisi niniaitwa Hawa Saad Bin Laden”

“Na Farida?”

“Ni jina langu la kazi, Farida Awadhi Amir, ila jina langu ni Hawa.”

Kwa haraka haraka nikaanza kupata fundisho kwenye maisha yangu kwamba sitakiwa kumuamini mwanamke kwa maana kwa jinsi alivyo niigizia huyu mwanamke kwa kweli ni jambo la kushangaza sana.

“Mimi ni mjukuu wa Osama Bin Laden, baaba yangu ni Saad Bin Laden ambaye alirithi madaraka ya babu yangu katika kikundi cha Al-quida miaka hiyo ya nyuma kabla ya mimi kushikilia madaraka hayo kwa sasa. Ninavyo zungumza hivi sasa hivi baba yangu ni marehemu naye ali uwawa na majeshi ya Marekani”

“Aisee pole sana mpenzi wangu”

“Nashukuru mume wangu, unajua ukiwa katika kundi kama hili hususani dunia linalifahamu kwamba ni kundi la kigaidi basi ni lazima macho ya nchi kubwa yatamtazama kiongozi wao na watahitaji wamuue, hususani Marekani ndio wenye kimbele mbele”

Farida alizungumza kwa sauti ya upole sana huku akinitazama usoni mwangu.

“Baba yangu alinikuza katika misingi ya kupigania haki na alinifanya kuwa mwanamke shujaa sana”

“Ngoja kwanza ilikuwaje ukaenda kuishi na mzee Khalid na ukamzalia watoto?”

“Njia salama ya mimi kukua na kufika umri maalumu wa kumiliki hili kundi hadharani sasa ni huu. Laiti kwamba Wamarekani wangefahamu juu ya uwepo wangu hakika wangeniangamiza mapema sana na nikiwa bado bini mdogo, kwa hiyo yuke mzee nilimtumia kama daraja langu la makuzi ya kufika hapa nilipo leo”

“Sasa watoto wako je?”

“Wataendelea kuishi kwa yule mzee, kwa maana siwezi kuwaingiza wanangu katika adha kubwa na ngumu kama hii ninayo iendea katika kuifanya. Randy natambua kwamba una maswali mengi sana, ila kadri siku zinavyo zidi kusonga mbele ndivyo jisni utakavyo kuwa ukinijua taratibu.”

“Sawa nimekuelewa kidogo, kuwa kiongozi wa kundi hilo ndio sababu ya wewe kujificha sura yako muda wote?”

“Ndio, isinge kuwa jambo rahisi kwa mimi kuiacha sura yangu kuonekana kwa kila mtu. Mzee Khalid pekee yeye ndio alikuwa akiiona sura yangu na halikuwa swala gumu sana kwangu kwa maana watu waliweza kufahamu kwamba hiyo ni moja wapo ya sheria katika dini yangu ya Uislam na mzee yule alikuwa akipenda sana kujisitiri kwangu, japo alikuwa akinipiga sana”

“Alikuwa akikupiga kisa nini?”

“Si unajua uonevu wa wanaume tu na ilinibidi niwe mvumilivu na niishi kwelli kama mwanamke ambaye sina msaada kwa mtu yoyote, ila laiti ningeamua kumkamua mzee yule iliikuwa ni kitendo cha sekunde moja ama mbili habari yake ingekwisha kabisa.”

Farida alizungumza kwa kujiamini sana.

“Kwa nini lihitaji nivunje sheria za jeshi ambalo nilijiunga?”

“Hilo jeshi unalo lizungumzia, mkuu wao yupo chini yangu, ni moja ya matawi ambayo tunayasaidia”

Hapa ndipo nikakumbuka kauli ya babu yangu kwamba alipata msaada wa kuanzisha kikundi chake kutoka kwa Osama Bin laden aliye kuwa kiongozi wake wa kikundi cha Al-quida.

“Hata barua ambayo nilikupatia, nilimueleza yule mzee aweze kukufwatilia kwa kila hatua ambayo una piga katika mazoezi na mtihani wako wa kwanza ilikuwa ni kujua je unaweza kunijali”

“Ngoja kwanza mpango wa mimi kutolewa nje na mwalimu wangu wa mazoezi ilikuwa ni mpango wako?”

“Ndio, na nilipenda ulivyo tumia akili nyingi, kwanza kubadilisha nguo, kutoa namba ya gari na maamuzi yako ya haraka kwa kila jambo linalo kuja mbele yako, hakika ulifaulu vizuri”

“Sasa kwa nini mwalimu wangu walimuua?”

“Ni mzembe, yupo kazini, ila ulevi na umalaya ukamponza, basi hapakuwa na jinsi zaidi ya kuuwawa kikatili na pia nilipenda zsana maamuzi ambayo uliyachukua ya kuto kurudi tena kambini na kuamua kutafuta njia nyingine ili mradi unilinde mimi mpenzi wako. Ndio maana nikasema kwamba wewe ndio mwanaume ambaye nilikuwa nikikuhitaji kwa pamoja nina imani kwamba tunaweza kuungana kwa pamoja na kulipiza kisasi kwa wale watu ambao waliwaangamiza wazazi wetu”

“Wazazi wetu kivipi?”

“Baba yangu na mama yangu waliuwawa na baba yako naye aliuwawa pia”

“Farida ngoja kwanza unataka kuniambia kwamba baba yangu ni marehemu?”

“Ina maana siku zote hufahamu kwamba baba yako ali uwawa?”

“Ndio!!’

Niliuliza huku nikiwa nimejawa na mshangao ulio ambatana na mstuko kwani siku zote nimekuwa nikikaa na kumuuliza mama yangu juu ya baba yangu, alinificha kumbe kuna siri hii ambayo Farida ana ifahamu.

“Ni nani aliye muua baba yangu?”

Niliuliza huku hasira ikianza kunipanda taratibu. Farida akanitazama kwa macho ya huruma huku akionekana kunionea huruma sana.

“Farida niambie ni nani aliye niua baba yangu”

“Anaitwa DANY……Alikuwa ni usalama wa taifa nchini Tanzania na baade akaisaliti nchi yake, akamua raisi K2 na pia ni miongoni wa watu aliye mua baba yako kwa kumchinja hadharani”

Machozi yaliyo ambatana hasira yakaanza kunimwagika usoni mwangu, hapa ndipo nikakumbuka maneno ya mama yangu kwamba lazima niwe jasiri ili aweze kuniambia baba yangu ni nani, kumbe kuna siri kubwa ya mauaji yake kama hii. Nikajikuta nikijiapiza kimoyo moyo ni lazima kwamba nimuue huyo Dany kama bado yupo hai.



“Randy mimi na wewe adui yetu ni mmoja, adui yetu ni Dany yeye ndio aliye tuulia wazazi wetu mume wangu”

Farida alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake, na kuzidi kuifanya jazba yangu kupanda na kuhitaji kuhakikisha kwamba ni lazima kwamba nina muangamiza huyo Dany.

“Una picha yake?”

Nilimuuliza Farida kwa sauti ya chini ila iliyo jaa mikwaruzo ya jazba.

“Ndio ninazo ila zipo makao makuu nchini Afghanstan”

“Tunakwenda lini huko?”

“Hadi kesho kutwa, tutakuwapo huko, japo ni safari ndefu”

“Nahitaji kumuona huyo mtu ana fananiaje?”

“Mume wangu, kwa ufupi huyo mtu ni gaidi wa dunia. Mtu huyo amefanya mambo mengi makubwa kuliko hata babu yangu Osama. Mtu huyo aliweza kumuua baba yako ambaye alikuwa ni raisi wa Marekani”

“Marekani?”

“Ndio, kwani mama yako hakuwahi kukueleza juu ya hilo?”

“Hapana, unaweza kunisaidia kupata laptop niweze kuiona japo sura ya baba yangu?”

“Mmmm ngoja”

Farida alizungumza na akashuka kitandani, akachukua taulo na kujifunga nusu ya mwili wake kisha akatoka humu ndani. Shauku ya kumfahamu baba yangu ikazidi kunijaa moyoni mwangu, ila japo nitamuona ila kusema kweli nitaumia sana kwa jinsi nilivyo simuliwa muaji yake kwa kweli ni jambo ambalo nitahakikisha kwenye maisha yangu, kulipiza kisasi ili mradi mama yangu aweze kuwa na amani.

“Na tumepewa na nguo”

Farida alizungumza huku akiingia ndani humu akiwa ameshika nguo zetu huku mimi nguo yangu ikiwa ni suti nyeusi na chati jeusi. Akafunga mlanngo na akaziweka nguo huzo kwenye moja ya kiti ndani humu kisha akaipanda kitandani akiwa ameshika laptop aina ya macbook air. Akaifungua na kuiwasha.

“Jina la baba yangu anaitwa nani?”

“Donald Bush”

Nikaingia katika mtandao wa Google na nikaandika jina la Donald Bush. Nikaletewa picha zake na historia yake ainayo onyesha mwaka alio zaliwa na mwaka alio weza kuuwawa kwa kuchinjwa. Nikaona picha zake akiwa na mama yangu Yemi kipindi wakiwa vijana. Nikaona picha za mama yangu akiwa mjamzito ambao ni wa mimba yangu. Machozi yakazini kunimwagika usoni mwangu.

“Baba yako alikuwa ni raisi wa Marekani, na yeye ndio alikuwa na ushirika mzuri na Osama Bin Laden, ila wote waliweza kuuwawa na Dany vifo vya kikatili sana”

“Picha ya Dany ipo wapi hapa?”

“Hata Google wenyewe hawana, sijui kuna kitu gani kilifanyika na picha zake zote zikafutika, ndio maana ninakuabia kwamba picha hizo zipo makao makuu, na baba yangu aliweza kuzihifadhi ili hata kama itakapo tokea kizazi chake kikikua basi tuweze kuona ni nani aliye husika na kifo cha babu yetu”

Farida alizungumza kwa sauti ya upole huku akinitazama usoni mwangu. Nikaendelea kuisoma historia ya baba yangu na mama yangu ambapo inaonyesha kwamba katika dhira waliyo itembelea nchi ya Tanzania, hiyo ndio iliwapelekea baba yangu kutekwa na kuuwawa na Dany huku mama yangu akiwa mikononi mwa gaidi huyo Dany.

“Ina maana huyu Dany pia alimuua raisi wa Tanzania Bi K2?”

“Ndio”

“Mmmmm”

“Mume wangu, ili kuweza kumpata Dany ni lazima tuhakikishe kwamba tuna mafunzo ya kutosha. Dany ni gaidi aliye tumia akili sana na cha kushangaza dunia ni kwamba hakuwa na jeshi kama ilivyo kuwa kwa magaidi wengine kama babu yangu, na watu wengine.”

“Mke wangu nitahitaji kumfahamu huyo Dany na nitahakikisha kwamba ninamuu kwa mkono wangu mimi mwenyewe”

“Randy…..”

“Lazima nimuue, hata iweje, nife mimi au afe yeye ni lazima nimuue”

Niliendelea kuzungumza kwa msisitizo huku nikimtazama Farida usoni mwake. Farida taratibu akanishika kifuani mwangu, mkoo wake akaupandisha hadi shavu la upande wa kulia na akaanza kunifuta taratibu machozi yangu. Tukatazamana kwa sekunde kadhaa, Farida akanisogezea lipsi zake na kuanza kuninyonyana lipsi zangu taratibu. Hisia za kimapenzi zikaanza kunipanda taratibu huku jogoo wangu naye akisimama dede. Farida akanishika jogoo wangu na kuanza kumchua taratibu na kunifanya hisia zangu za mapenzi zizidi kupanda maradufu. Nikaanza kunyonya maziwa ya Farida na kumfanya kuanza kutoa miguno ya kimahaba. Tukaanza kupeana burudani iliyo pelekea shuka lililo tandikwa kuchanguka changuka hadi laptop nayo ikaanguka chini, ila hatukulijali hilo hadi tulipo hakikisha mzunguko wetu wa kwanza unaisha, huku kila mmoja jasho likimwagika usoni mwake.

“Randy tumefunja laptop ya watu”

Farida alizungumza huku akiiokota laptop, kwa bahati nzuri haikuweza kuvunjika wala kupata madhara ya aina yoyote.

“Mmmm wewe mwanaume sikuwezi”

“Kwa nini?”

“Yaani unanifanya kila muda nitamani kupata penzi lako”

“Nikuambie siri moja?”

“Siri gani?”

“Ila hato kasirika?”

“Niambie tu, siwezi kukasirika”

“Kipindi kabla sijakupata wewe, nilikuwa siwezi kufanya mapenzi na mwanamke mmoja. Kiufupi mwanamke mmoja alikuwa anitoshelezi ila wewe kusema ukweli unanitosheleza hadi ninaanza kukuogopa”

“Kwa nini unaniogopa?”

“Sijawahi kumpata mwanamke ambaye anaweza kunihimili, aikiwa mmoja basi ni lazima atapoteza fahamu”

“Duuu pole yao, ila niahidi kitu kimoja Randy”

“Kitu gani?”

“Utanioa na hato niacha?”

“Siwezi kukuacha Farida, nikikuacha wewe nitaendelea kuwatesa wanawake wengine katika swala zima la kitandani”

“Una uhakika na unacho kizungumza?”

“Asilimia mia moja”

“Randy kumbuka kazi tunayo iendea ni kubwa, si kazi ya kitoto na wala si kazi ambayo sisi kama sisi, tuwe tunagombana kwa ajili ya maswala ya wivu. Haki ya Mungu, Randy nikifahamu una mwanamke mwengine nitahakikisha kwamba nina muua huyo mwanamke pasipo huruma ya aina yoyote”

“Usijali mke wangu”

“Wewe sema tu hivyo, mimi nina roho mbaya sana Randy na nina penda. Nikipenda nina penda sana”

“Usijali mke wangu”

Tukarudi bafuni na kuoga, tukavaa nguo tulizo andaliwa na kutoka ndani humu. Farida akanitembea katika eneo zima la nyumba hii. Majira ya usiku tukatoka chakula cha jioni na kuelekea kwenye moja ya hoteli kubwa ya kitali.

“Umeipenda hii hoteli?”

“Yaa nimeipenda mke wangu pazuri sana”

Nilizungumza huku nikitazama walinzi wa Farida tulio kuja nao hapo hotelini wakiwa wamezagaa katika eneo hili, huku wakiwa makini sana katika kutulinda.

“Kwa nini unatembea na walinzi wengi hivi, moja, bili, tatu…..”

Nilizungumza huku nikihesabu idadi ya walinzi hao na kuwakuta wapo kumi na bili

“Kwa ajili ya usalama wangu, unajua hadi sasa hivi nchi kama Marekani kama nilivyo kuambia kwamba wana niwinda kwa maana wanataka kufyeka kizazi cha baba yangu ambaye alikuwa ndio mreisi wa kundi la Al-quida ndio maana hata kule Niger waliweza kunitambua baada ya kuipata picha yangu”

“Sasa kwa nini hukuniambia mapema ili meneja asikupige zile picha?”

“Wazo hilo nilikuwa nalo ila sikuhitaji kujidhihirisha mapema, nilihitaji kukusaidia pale utakapo kuwa umeshindwa kabisa nami nikuonyeshe kwamba nami nina uwezo, ila mambo yakaharibika ila niliweza kujianda kwa tukio lile na kweli likatokea”

“Mmmm sawa”

“Tuachane na hayo mambo yamesha pita. Ehee hembu niambie maisha yako ya Nigeria yalikuwa ya aina gani na ni kina nani walikupiga risasi?”

“Ni historia ndefu kidogo mke wangu. Unajua mama yangu toka nilipo kuwa mtoto mdogo hakuwa na furaha na mimi, alikuwa ni mkali sana kwangu. Sikujua ni kwa nini yupo vile. Hadi ninakuwa mtu mzima yeye yupo vile vile na inapekekea maisha yangu kuwa kama hivi yalivyo kuwa”

“Ehee na walio kupiga risasi?”

“Kuna mfanyakazi wangu mmoja wa kike nilikwenda naye kwake mara baada ya kuacha kazi ofisini kwa mama. Mpenzi wake aliye achana naye alikuwa ni mwanajeshi, basi alikuja akanikuta ndani mule na kwa bahati nzuri sikuwa na hisia na yule sasa. Yule mwanajeshi katika kuanzisha fujo za hapa na pale kwa bahati mbaya akaangukia meza ya kioo ikapasuka na ikamchoma.”

“Kabla ya ajali hiyo, asubuhi nilizungumza na mkuu wa jeshi na kumuomba nafasi ya kujiunga na jeshi lake, sasa baada ya ajali hiyo nilihisi mkuu wa jeshi atanisaidia, ila kwa bahati mbaya alinigeuka na aliwahitaji vijana wake waniue na kweli walinipiga risasi, hivyo nahisi huko watakuwa wanahisi kwamba nimekufa”

“Mmmm sasa kosa la yeye kukusaliti hadi akuue ni nini jamani?”

“Alidai kijana wake niliye muua alikuwa ana kwenda kuwa komandoo. Ila kwa akili yangu ya haraka haraka nihisi kuna sababu nyuma ya pazia”

“Mmmmm pole sana, ila tutalishuhulikia”

“Achana nao kwa maana Mungu amenisaidia hadi sasa sijakufa basi hakuna haja ya kuendelea kulishuhulikia”

“Ila siku wakifahamu kwamba upo hai watakutafuta na kumbuka wakikutafuta si kama watakuja kukushangaa, ila watakuja kwa ajili ya kukua”

“Wewe kama wewe unahitaji tuwafanye nini?”

“Tuwashuhulikie”

“Basi hilo swala tutalifanya baada ya mimi kuwa kamili kwenye mafunzo”

“Sawa”

“Ila kuna jambo moja nahitaji unisaidie kabla sijalisahau”

“Jambo gani?”

“Kuna yule mkuu wa kile kikundi cha kijeshi alikuja vijana”

“Okay”

“Kwa haraka haraka aliniambia kwamba ni baba yangu mdogo, alizaliwa tumbo moja ba babu mzaa mama, sasa sikupata nafasi ya kumuona toka siku ile tulivyo zungumza”

“Usijali ni mmoja wa wanachama wangu, na ni kweli mama yako anamuita yule mzee baba mdogo, ila hawajakutana siku nyingi”

“Farida kama unaifahamu historia yangu kwa ukamilifu nakuomba uniambie yote, unajua katika kukua kwangu kote ninamjua mama tu ila sijawahi ona mama mdogo, mjomba babu wala baba”

“Taratibu tu mke wangu utayajua mambo mengi, wala usijali katika hilo”

“Kweli?”

“Ndio, tufurahie maisha ya hapa na kesho tutaondoka hapa na tunaendelea na safari yetu”

“Sawa”

Siku ya leo kwangu kwa namna moja ama nyingine ni siku ya niliyo fahamu mambo mengi ambayo yameanza kunipa mwanga kwenye maisha yangu ya sasa na ya baade. Tulipo maliza kupata chakula cha usiku na tukaelekea kwenye moja ya ukumbi wa starehe. Tukasherekea katika ukumbi huo kwa muda kama wa masaa matatu kisha tukarudi nyumbani huku tukiwa tumechoka na kunywa pombe nyingi sana. Kutokana na kuchoka na kulewa sana, kitendo cha kuingia ndani, tukajikuta usingizi mzito ukitupitia na tukalala usingiiz fofofo.

Asubuhi nikawa mtu wa kwanza kuamka, nikamuamsha Farida na tukaingia bafuni na kusafisha vinywa na miili yetu.

“Muda umekwenda sana ehee?”

Farida ainiuliza huku akisugua meno yake na mswaki.

“Yaa umekwenda”

“Duu tutachelewa ndege”

“Kwani ilipangwa tuondoke muda gani?”

“Saa nne asubuhi”

Nikachungulia chumbani na nikaitazama saa iliyopo ukutani.

“Sasa hivi ni saa tatu kasoro dakika ishirini”

“Mmm afadhali kwa maana nilihisi ni saa tatu na tiketi mjomba amesha tukatia”

“Hivi tutazirudia nguo hizi hizi?”

“Hapana nitakwenda kuchukua nyingine.”

Tukarudi chumbani huku tukiwa tumemaliza kuoga huku kila mtu akiwa na haraka. Farida akatoka ndani humu na baada ya muda akarudi akiwa amebeba kanzu, baibu.

“Hee ninavaa kanzu?”

“Ndio, nchi tunazo kwenda, haya mavazi yametawala sana, hivyo ni lazima tuweze kuyavaa ili tuweze kuendana na watu wa huko, kofia hiyo hapo na suruali ya kuvaa ndani ya kanzu hiyo hapo”

Farida alizungumza huku akiniwekea nguo hizo kitandani. Sikuhitaji kuuliza maswali mengi zaidi, nikaanza kuvaa haraka haraka. Tulipo maliza tukatoka ndani ya chumba hichi na kuelekea katika meza ya chukula, tukapata kifungua kinywa na safari ya kuelekea uwanja wa ndege ikaanza huku tukiwa tumeongozana na gari mbili zenye walinzi. Tukafika katika kiwanja cha ndege kiitwacho Tripol Intertional Airport. Tukashuka kwenye gari na tukaagana na mjomba kisha yeye na walinzi wakarudi kwenye magari na sisi tukaingia ndani. Moja kwa moja tukaelekea kwenye sehemu ya kukaguliwa hati zetu za kusafiria, zikapigwa mihuri kisha tukaelekea katika basi maalumu lililo tupeleka hadi kwenye ndege ya shirika la Libyan Airlines. Tukakaa kwenye siti zetu na kusubiri safari iweze kuanza.

‘Mungu naomba utuongoze kwenye safari hii’

Niliomba kimoyo moyo kwa maana hii ni safari nyigine ambayo sijui huko ninapo elekea papo vipi.

“Randy”

Niambie mume wangu?”

“Ninakupenda sana”

“Ninakupenda pia mke wangu”

“Kweli”

“Ndio”

Farida taratibu akakilaza kichwa chake kwenye bega langu la mkono wangu wa kulia huku tukisubiria ndege hii ianze safari rasmi. Abiria wakaendelea kuingia na kukaa kwenye siti zao, taratibu nikashuhudia ndege hii ikianza kuondoka kwa mwendo wa taratibu, ila gafla ndege hii ikasimamsa jambo lililo wafanya hata abiria wengine kushangaa, nikatazama nje kupitia kioo nikaona gari zaidi ya kumi za CIA wakilizunguka gari hili jambo lililo nifanya nistuke sana na nikamgusa Farida pajani.

“Vipi baby”

“Angalia nje?”

Farida akatazama nje, akastuka sana.

“Randy nilazima tutoke kwenye hii ndege kwa maana wametufwata sisi”

Farida alizungumza huku mapigo ya moyo yakimuenda mbio na mkono wake mmoja akifungua mkanda wa siti tayari kwa kunyanyuka na kutafuta njia ya kuweza kutoka ndani ya ndege hii kabla ya kingia mikononi mwa wana usalama wa kikosi cha Kimarekani cha CIA.



Kwa haraka na mimi nikafungua mkanda wa siti yangu huku macho yangu yote nikitazama nje jinsi askari wa CIA wakiwa wameshikilia bunduki zao.

“Tutatokea wapi mke wangu?”

Nilimuuliza Farida kwa sauti ya chini huku nikimtazama usoni mwake. Farida kwa haraka akasimama na kuanza kutembea kuelekea kwenye chumba ambacho wakaaa wahudumu wa ndege hii. Nikaanza kumfwata kwa nyuma, nikamkuta akizungumza na mmoja wa wahudumu.

“Yaa wanadai kwamba watu hao wamo humu ndani ya ndege?”

Niliikutia hapo sentensi ya muhudumu huyo wa kike.

“Wamewatajia ni watu gani?”

“Wanasema ni wanaume wawili hivyo tunawaomba muweze kurudi kwenye siti zenu na mutulie kila kitu kitakwenda vizuri.”

Akaongezeka na mzee mwengine wa kizungu huku naye akionekana kwamba ana shahuku ya kuhitaji kuweza kufahamu ni kitu gani kinacho endelea. Farida akanitazama usoni mwangu, kwa ishara ya macho akaniomba turudi kwenye siti zetu. Tukarudi na kukaa huku tukiifinga mikanda yetu.

“Una uhakika na maamuzi haya?”

Nilimuuliza Farida kwa sauti ya chini.

“Ndio mpenzi wangu ila tuwe makini”

“Sawa”

Taratibu tukashuhudia mlango ukifunguliwa. Baada ya dakika kama mbili hivi wakaanza kuingia wana CIA huku wakionekana kuwa makini sana. Kiongozi wa kikosi hichi akaingia kwenye chumba cha wafanyakazi wa kike na baada ya muda kidogo tukaisikia sauti yake ikitutangazia.

“Habari zenu abiria. Sisi ni The Central Intelligence Agency, tunawaomba abiria musiwe na wasiwasi, ndani ya muda mfupi zoezi letu lililo tuleta litakamilika, asanteni”

Wana usalama hawa wakaanza kukagua mizigo yote iliyo chomekwa katika sehemu maalu ya mizogo katika ndege hiii. Enao la juu la siti zetu zilipo mimi na Farida, wakatoa brufcase yenye rangi ya silver.

“Ohoo Mungu wangu”

Alizungumza Afisa huyu huku macho yakimtoka.

“Tunawaomba musegee kwenye hii siti”

Alizungumza afisa huyu, kwa haraka tukafungua mikanda yetu na kusimama pembeni, nikatizama eneo ilipo tolewa brufcase hiyo na nikashuhudia bomu la kutegwa, likiwa limesalia dakika tatu kabla ya kulipuka, mwana usalama mmoja akanikonyeza nisizungumze chochote ili kuto wapa abiria wengi presha. Farida naye akaweza kuliona bomu hilo macho yakamtoka ila nikawahi kumshika mkono wake wa kulia na kuuminya kidogo ili naye asizungumze kitu chochote. Wanausalama wawili, wakapanda juu ya siti zetu, huku wakiwa na vifaa maalumu.

“Ni nini?”

Bibi mmoja wa siti ya pembeni aliuliza huku akihitaji kusimama, ila mwana usalama mmoja akamzuia na kumuomba asisimame.

“Kila kitu kinakwenda kuwa sawa bibi”

Mwanausalama huyo alizungumza huku wezake wakiendelea kujitahidi kulitegua bomu hilo. Dakika zikazidi kusonga mbele ila suluhisho la kulitegua bomu hilo bado halijapatikana.

“Watatuulia humu ndani”

Farida alizungumza kwa sauti ya kuninong’oneza huku tukitazama bomu hilo linalo onyesha kwamba zimesalia dakika moja na sekunde thelathini kabla halijalipuka. Farida akamfwata mwana usalama mmoja na kuanza kuzungumza naye kwa sauti ya chini. Sikuweza kuelewa anazungumza naye nini. Mwana usalama huyo akawasiliana na mkuu wake kwa kutumia kifaa maalumu cha mawasiliano yake alicho kifungu sikioni mwake. Mkuu wake kwa haraka akafika sehemu walipo simama na Farida, wakazungumza kidogo kisha Farida na mkuu huyo wakafika katika siti zetu.

“Vipi?”

Mkuu huyo aliwauliza vijana wake.

“Hakuna utatuzi mkuu”

“Hembu mpeni nafasi huyu dada”

Bomu hili limebakisha sekunde hamsini na tano hadi lilipuke, vijana hawa wakashiuka na akapanda Farida, hapa ndipo baadhi ya abiria walipo gundua kwamba ndani ya hii ndege kuna bomu la kutegwa. Farida akachukua vifaa walivyo vitumia vijana hao na kuanza kulishuhulikia bomu hili. Sekunde zikazidi kupungua na kubaki sekunde thelathini, nikamuona jinsi Farida anavyo tetemeka mikono huku jasho likimwagika mikononi mwake.

‘Ehee Mungu watu tusaidie’

Nilisali kimoyo moyo kwani kushindwa kwa Fardia basi watu wote tulipo ndani ya hii ndege ni lazima tufe kwa kulipuka. Sekunde zikasalia ishirini, ila bado Farida hajafanikiwa, mapigo ya moyo kwa upande wangu nayo yakazidi kunienda kasi kwani katika umri wangu huu mdogo bado sijawaza wala kufikiria kitu kinacho itwa kifo, japo hakuna anaye jua ni lini atakufa, ila kifo hichi cha kushuhudia kwa kweli kinauma. Nikawatazama wana usalama wengine nao nyuso zao zinaonyesha kujawa na mashaka makubwa sana. Hadi inafika sekunde ya pili kabla ya kulipuka, bomu hilo likasimama. Nikamuona Farida akishusha pumzi nyingi sana, kwa haraka nikamkimbilia na kumkumbatia kwa nguvu na kuwafanya abiria baadhi kusimama huku wakishangaa shangaa.

“Umefanikiwa mke wangu”

“Ndio baby”

Farida alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake. Wanausalama wakapanda kwenye siti zetu na kulifungua bomu hilo. Wakalitoa na wakatutangazia abiria wote kwamba ndege kwa sasa ipo salama na tunaweza kuendelea kwa safari.

“Tunashukuru kwa msaada wako na pia tungependa kufahamu mambo macheche juu yako, na ikiwezekana tuweze kuwa nawe?”

“Kwa ufupi mimi ni specialist wa mabomu na ninafanya kazi chini ya serikali yangu ya Saud Arabia, hivyo labda muniachie namba zenu ili nikifika Saud Arabia basi muweze kuwasiliana na mkuu wangu wa kazi”

“Sawa”

Mkuu huyo wa kikosi chihi cha CIA, akatoa kitabu kidogo mfukoni mwake, akachomoa kalamu kwenye mfuko wake wa shati, akaandika namba na kumkabidhi Farisa.

“Asanteni sana”

Farida alizungumza hukua kikikunja kikaratasi hicho vizuri.

“Karibuni sana”

Abiria wote wakapiga makofi na kumpongeza Farida kwa juhudi alizo zifanya za kutuokoa. Muhudumu kwa haraka akaizifuta uchafu siti zetu na kwa heshima sana akatukaribisha tuweze kukaa na kuendelea na safari yetu.

“Hongera sana binti”

Bibi aliye kaa siti ya jinani na sisi alizungumza huku akimkabidhi Farida mkono, Farida akaupokea mkono wa bibi huyo huku akitabasamu. Baadhi ya abiria wakendelea kumpongeza Farida na baada ya wanausalama wote wa CIA, kutoka katika ndege hii, taratibu ndege ikaanza safari yake na baada ya muda mchache ikaacha ardhi ya Libya na kupaa angani.

“Mke wangu kumbe una ujuzi mkubwa kama huo hujawahi kuniambia”

“Usijali mume wangu, kuna mambo mengi sana utaweza kuyafahamu kupitia mimi”

“Hili swala la kufanya kazi katika serikali ya Saud Arabia ni kweli?”

“Ndio, ila tukipata muda mpenzi wangu tutazungumza”

“Sawa”

“Ila huyu mshenzi aliye fanya hivi nimemfahamu na nilazima nimuazibu”

“Ni nani?”

“Nitakuambia”

Farida alinijibu kwa msisitozo huku macho yakiwa yamemtoka kwa hasira. Taratibu nikakilaza kichwa begani mwangu, ili kumtuliza jazba yake. Tukafika nchini Misri, ndege ikashusha baadhi ya abiria na wakapanda wengine na safari ikaendelea.

“Umechoka mume wangu?”

“Kiasi”

“Sio sana?”

“Kiasi kidogo japo tumekaa masaa mengi sana”

“Pole mwaya, sasa tukitoka hapa Misri, tunaliacha bara la Afrika na kuelekea barala la Asia”

“Ila kwenu ni mbali kwa kweli?”

“Yaa ni mbali, ila ndio maana zikabuniwa hizi ndege. Pata picha watu wangekuwa wanasafiri kwa magari ingekuwaje”

“Mmmm nahisi gari zima lingejaa madereva kwa maana kusinge kuwa na dereva mwenye ubavu wa kuendesha kwa mwendo mrefu kiasi hicho”

“Ni kweli. Huko tunapo kwenda tutafikia kwenye mji mmoja unaitwa Riyath. Mji huo ndipo alipo zaliwa babu yangu”

“Ahaaa”

“Yaa hapo ndipo ilipo asili ya okoo wangu wa Bin Laden”

“Nikuulize swali mke wangu?”

“Uliza?”

“Hivi hawato nichukia kuniona mimi, kwa maana inavyo fahamika warabu nyinyi munapenda kuolewa au kuoana ninyi kwa ninyi?”

Farida akaka kimya huku akionekana akitafakari swali langu.

“Dunia kwa sasa imebadilika, hilo swala kweli lipo toka miaka mingi sana ya nyuma. Ila kutokana na utandawazi basi, mambo yamekuwa mchanganyiko na wala sidhani kama itakuja kutokea mtu akapinga mahusiano yetu japo sisi ukoo wetu ni watu wa dini sana na kama itawezekana ili tuweze kuishi kwa amani inabidi ubadili dini?”

“Dini…..!!?”

Niliuliza huku macho yakinitoka.

“Ndio mume wangu, watu wengi kwenye ukoo wangu wanaangali dini. Lazima uwe muislam, ujua Uislam ndio maana hata tukipigana tunapigana kwa ajili ya dini”

Farida alizungumza kwa sauti ya chini ambayo hakuna mtu mwengine ambaye anaweza kuisikia. Nikabaki na bumbuwazi, kwani kwenye maisha yangu sijawahi kufikiria siku hata moja kubadilisha dini yangu, japo sio muhudhuriaji wa kanisani sana, ila kiimani nina amini katika ukirsto.

“Nalitambua hilo ni gumu sana kwako mume wangu, ila inabidi iwe hivyo. Huko tunapo kwenda ukristo ni mdogo sana na wengi wao wapo hatarini sana kimaisha. Wengi wao huambulia kunyongwa na wengine kulipuliwa wakiwa makanisani mwao. Japo si kindi langu, ila vipo vikundi vidogo vidogo vina msimamo mkali wa kidini ndio vinafanya matukio hayo mabaya”

“Mke wangu”

“Beee”

“Au basi”

“Hapana zungumza tu Randy wangu, mimi nipo kwa ajili yako na mimi ndio ninaye kupenda. Kuwa muwazi na zungumza mimi nitakuelewa, ila nimezungumza hivyo ili kukuelewesha, ili uweze kufahamu kwamba sehemu hizo tunazo ziendea sio za kawaida sana”

“Nimekuelewa mke wangu, ila nilihitaji kusema kwamba, je ikitokea nika kataa kubadilisha dini yangu?”

“Mmmmm. Utaniweka mimi katika wakati mgumu, japo kweli nina nguvu, ila wale ninao waongoza ndio wananifanya mimi niwe na nguvu, bila ya kuwa nao na amani, mambo yatatokea kama haya”

“Yapi?”

“Huyu aliye weka bomu hili, au bomu hili lililo kuwa limetegwa kwenye hii ndege, ni miongoni mwa wataalamu wezangu. Mtu huyu toka nilipo kuwa mdogo alikuwa akinipenda kimapenzi, na kama unavyo sema kwamba tuna aona sisi kwa sisi, ila naamini kwamba amesikia nimepata mwanaume tena wa kiafrika, ndio maana aliamua kutega hili bomu ili mradi aniue, ila kutokana ameshindwa basi ni lazima nimuwahi yeye kabla hajatumaliza”

Mwili mzima ukanitetemeka, kwa maana kama watu wanahitaji kuniua kwa ajii ya Farida basi huko niendapo sio salama kabisa kwa maisha yangu.

“Ndio maana sikuhitaji kukuambia toka tulipo kuwa tuna ianza safari kule Libya, nilijua utajawa na wasiwasi, ila tambua kwamba upo nitakulinda kwa maisha yangu yote Randy, nina kupenda na kukuhitaji zaidi ya unavyo fikiria mpenzi wangu”

“Farida”

“Beee”

“Ikitokea wakawahi kukumaliza wewe na mimi nikabaki, hivi itakuwaje, nitafanikiwa kweli kumaliza kazi yangu ya kulipa kisasi?”

Farida akaka kimya huku akionekana dhairi kwamba amekosa jibu la kunijibu.

“Niambie mke wangu je kweli nitaweza?”

Nilizungumza huku machozi yakinilenga lenga usoni mwangu.

“Randy, nilazima uwe jasiri, ni lazima uwe mpambanaji, usiogope kifo. Kifo kipo kwa ajili yetu sote. Unapo pata nafasi ya maisha, unapo pata nafasi ya kufanya jambo fanya pasipo kungoja kesho, kwa maana hakuna hata mmoja wetu ambaye ataifikisha kesho yake wala uiona.”

Farida alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake. Taratibu Farida akanikumbatia kidogo.

“Ninakupenda Randy, hakikisha unapo pata nafasi ya kijasusi unajifunza kikamilifu ili hata ukiwa peke yako pasipo uwepo wangu basi unafanya kikamilifu saawa mume wangu”

“Sawa mke wangu”

Tukafika nchini Saud Arabia katika kiwanja cha King Khalid International Airport majira ya saa kumi na moja Afajiri. Tukatoka katika kiwanja hichi, tukakuta gari moja aina ya Range Rover ikitusubiria nje, tukaingia ndani ya gari ambapo dereva wake amevaa suti nyeusi na miwani nyeusi.

“Boss karibu”

“Nashukuru, Jabir yupo?”

“Ndio mkuu yupo kwake”

“Nipeleke kwake”

“Sawa”

Farida alitoa maagizo hayo kwa kijana huyu mwenye ndevu nyingi usoni mwake.

“Mume wangu karibu na usiogope sawa, mji huu ni salama kwa kila aingiaye na atokaje”

“Sawa mke wangu”

“Nipatie bastola yako ya ziada”

Farida alizungumza na kijana wake huyo akachomoa bastola na kumkabidhi. Farida akatoa magazine ya bastola hiyo akaitazama na kukuta ina risasi za kutosha, akairudisha magazine na kuikoki vizuri.

“Ya nini hivyo bastola?”

“Kwa ajili ya kujilinda tu mume wangu. Samir umemueleza mtu yoyote juu ya ujio wangu?”

“Hapana Madam nimefanya kama ulivyo niagiza”

“Sawa sawa. Alafu Samir huyu ni mume wangu, hakikisha kwamba anapata ulinzi wako muda wowote na popote atakapo hitaji kwenda”

“Nimekuelewa mkuu nitafanya hivyo”

“Nashukuru sana”

Gari likaendelea kusonga mbele huku tukikatiza katika mitaa iliyo jengwa viruzi kwa magorofa mazuri na nyumba nzuri sana.

“Mjii huu ni mzuri sana mke wangu”

“Yaa ni mzuri, tutatembea baade usiku kama tukipata muda mzuri”

“Sawa mke wangu nitafurahi kwa maana majengo haya sijawahi kuyaona Nigeria wala Niger”

“Usijali mume wangu”

Gari likasimama mbele ya nyumba moja nzuri. Tukashuka sote ndani ya gari huku Nasir akiwa nyuma yetu. Tukafika mlangoni na Farida akagonga mlango huu. Baada ya muda kidogo tukaanza kusikia vishindo vya mtu akitembea akija mlangoni hapa. Kwa haraka Farida akachomoa basto aliyo pewa na Nasir. Kitendo cha mwanaume huyo kufungua mlango, Farida akampiga na kitako cha bastola hii usoni mwake na mwanaume huyu akaanguka chini mzima mzima, jambo lililo nifanya nishangae sana, kwani mke wangu sio mtu wa mchezo mchezo.



“Farida nini unafanya?”

Mwanaume huyu aliye valia kanzu alizungumza huku macho yakiwa yamemtoka sana.

“Ulijua tutakufa si ndio?”

“Una maanisha nini Farida?”

“Acha kujitia hufahamu ujinga ulio ufanya Jabir”

Farida alizungumza huku akiwa amekazia macho jamaa huyu ambaye hadi sasa hivi sijui ni nani kwake na kwa nini wanazungumza mazungumzo hayo.

“Farida mpenzi wangu, mimi sitambu ni nini unacho kizungumzia”

Farida bila ya huruma akamtandika risasi ya mguu mwanaume huyu na kumfanya atoe ukelele mmoja mkali sana hadi nikaogooa nikahisi labda kuna watu wanaweza kuingia ndani humu.

“Kwa nini utume watu waweke bomu kwenye ndege eheee?”

Farida aliendelea kuzungumza kwa ukali, hapa ndipo nami nikagundua kwamba huyu kumbe ndio yule mwanaume aliye sema ana wivu dhidi ya penzi letu.

“Bomu, bomu gani Fairda?”

Jafar aliendelea kuzungumza kwa sauti ya majonzi huku akimtazama Farida usoni mwake.

“Hujui si ndio?”

“Ndio”

“Nasir hakikisha kwamba ana zungumza ukweli”

Farida akapiga hatua kadhaa nyuma. Nasiri bila ya huruma akampiga teke Jafar la kifuani mwake na kumfanya jaama kuanguka chini. Nasir akachukua bastola yake na kuanza kuigandamiza kwenye kidonda cha Jabir na kumfanya jamaa kulia kama mtoto mdogo.

“Jabir unanijua sina roho ya huruma toka utotoni, na bomu lililo kuwa limetegwa kwenye ndege ni mtu mmoja tu ambaye anaweza kulitengeza duniani na ni wewe kwa maana nimeona code namba yako ya 9688”

Farida alizungumza huku akichuchumaa mbele ya Jabir anaye endelea kuminywa kidonda chake.

“Zungumza ukweli na usinidangaye”

“Farida hivi unahisi nitakubali kuona kwamba unaolewa na huyo mtu mweusi si ndio?”

“Ndio ukaamua uniue mimi na yeye na abiria wengine waiso na faisi si ndio?”

Jabir hakujibu kitu chochote. Farida akampiga risasi ya kichwa Jabir na akaanguka chini na damu taratibu zikaanza kuzagaa kwenye sakafu.

“Hakikisha kwamba unasafisha eneo hili. Ninaomba funguo”

Samir akamkabidhi Farida funguo kisha tukatoka nje ya nyumba hii, sikuweza kuona hata jirani mmoja ambaye ametoka kusikiliza na kufahamu ni kitu gani ambacho kinaendelea kwa jirani yao. Tukaingia ndani ya gari na kuondoka eneo hili.

“Sikupanga kumuu mtu leo ila huyu mpumbavu ameingia kwenye kumi na nane zangu”

“Huyu alikuwa nimpenzi wako?”

“Utotoni”

Farida alinijibu kwa ufupi huku akiendelea kuendesha gari hili kwa kasi. Tukafika kwenye jumba moja kubwa ambalo nje tukakuta walinzi walio valia nguo za kijeshi na wamezungushia vitamba vikubwa vya rangi rangi kwenye shingo zao. Wakampigia saluti Farida na gari likaingia ndani taratibu.

“Hapa ni wapi mke wangu?”

“Hapa ni makao makuu ya kutengo changu ninacho fanyia kazi kama mpelelezi wa kiserikali, nimekuja kuwakilisha ripoti yao walio kuwa wamenitum”

“Ngoja kwanza mke wangu mbona sikuelewi, umesema wewe ni mkuu wa kikundi cha Al-quida, saa hivi una sehe ni mpelelezi wa serikali sasa hapo nikuelewe vipi?”

“Mume wangu, tambua kikosi cha Al-quida sio serikali, kina lindwa kila kona na kina tafutwa kila kona na pasipo mimi kutumia akili ya ziada mkeo leo hii ningekuwa ni marehemu”

“Sawa mke wangu, nimekuelewa katika hilo, ila inakuwaje unafanya kazi mbili kwa wakati mmoja?”

“Serikalini nipo kwa ajili ya kupata kile ninacho kuhitaji, nimesha kimaliza kukipata nakuhakikishia kwamba nitakuwa nawe pamoja. Nakuomba unisubiri nahitaji kupandisha juu gorofani mara moja nitarudi baada ya dakika kumi na tano”

“Sawa mke wangu, ila kuwa makini huko uendapo?”

“Usijali mume wangu, nipo makini zaidi ya unavyo fikiria”

“Sawa”

Farida akanibusu mdomoni mwangu, kisha akashusha kwenye gari na kunifanya nishushe pumzi nyingi sana kwani hadi sasa hivi kwa kweli bado sijamuelewa huyu mke wangu. Nikaendelea kukaa ndani ya gari hili huku nikiangalia magari yanayo ingia na kutoka kwenye jengo hili analo dai ni la usalama wa taifa la hapa Saud Arabia. Ulinzi katika eneo hili kusema kweli ni mkali sana, na hakuna anaye ingia pasipo kukagulia, kwa vifaa maalumu, ila ni mimi tu ndio nimeweza kuingia pasipo kukaguliwa, yote ni kutokana nipo na mkuu wao.

Dakika kumi na tano zikakatika na Farida hakuweza kutoka, nikaendelea kusubiri hadi lisaa moja likapita ndipo nikamuona akitokae kwenye mlango alio kuwa ameingilia huku akiwa ameongozanana mzee mmoja mwenye ndevu nyeupe. Wakafika katika gari hili na wakaingia wote huku mzee huyu akikaa siti ya nyuma.

“Samahani mume wangu kwa kuchelewa kufika hapa”

“Usijali mke wangu”

“Mzee wangu huyu ndio kijana ambaye nimekueleza juu juu. Ni mume wangu mtarajiwa”

“Karibu sana Saudi Arabia kijana”

“Nashukuru sana mzee wangu”

“Mume wangu, huyu ni mshauri wangu kwenye mambo yangu mengi sana na pia ni mkuu wangu wa upelelezi na amenikuza kama mwanaye wa kike anaitwa mzee Suleiman Abud.”

“Kijana karibu sana, kwa sasa munawea kwenda nyumbani kupumzika, jioni nikitoka kazini nitapitia hapo nije kuwatembelea”

“Nashukuru sana mzee wangu”

“Farida hakikisha muna kuwa salama”

“Sawa mzee wangu”

Mzee huyu akanikabidhi mkono huku akinitazama usoni mwangu kisha akashusha kwenye gari. Farida akawasha gari na taratibu akaligeuza na tukaanza kuelekea getini.

“Mbona upo kimya mume wangu?”

“Nina maswali mengi sana juu yako ya kukuuliza”

“Usijali mume wangu niulize tu”

“Nahitaji tukiwa tumetulia ndio nikuulize”

“Sawa sawa”

Safari yetu ikaendelea hadi kwenye moja ya gorofa. Tukaingia kwenye lifti na kuanza kupandisha gorofani huku mimi nikiwa nimebeba kibegi kidogo chenye hati zetu za kusafiria pamoja na pesa za matumizi. Tukafika gorofa ya tisa, lifti ikafunguka na tukaanza kutembea kwenye kordo moja ndefu yenye milango mingi iliyo funga. Tukaifka kwenye moja ya mlango wa mwisho, Farida akachuchumaa chini kidogo na kutoa funguo kwenye chungu kilicho oteshewa ua kubwa na zuri. Akafungua mlango na tukaingia ndani.

“Karibu sana mume wangu, hapa ndipo ninapo ishi nikiwa hapa Saudi Arabia”

“Asante”

Nilijibu kwa ufupi huku nikikaa kwenye moja ya kiti.

“Ila mbona kama unaonekana huna furaha mume wangu?”

“Hivi kwa nini unapenda kunieleza maisha yako nusu nusu eheee?”

“Lakini Randy…..”

“Hakuna cha lakini, umekuw ni mtu wa kunidanganya kwa nini lakini?”

Nilizungumza kwa hasira huku nikimtazama Farida usoni mwake.

“Mume wangu nakuomba uweze kunisikiliza tafadhali”

Farida alizungumza kwa sauti ya chini sana huku akinitazama usoni mwangu. Akanisogelea na kunishika kiono changu.

“Randy, muda mwingine katika maisha ni lazima kuna baadhi ya vitu ujifunze kuweka ni siri, hata kwa mke wako. Mimi niliingizwa kwenye kikosi cha usalama wa taifa hili, nikiwa na umri mdogo sana. Yote ni kutokana na uwezo wangu wa kiakili. Niliweza kupokea mafumo ya kijasusi na nilikuwa ni miongoni mwa watengenezaji wa mabomu. Hata kwenda kuishi nchini Niger, niliishi kutokana na kazi maalumu iliyo nipeleka pale na nilifanikiwa kuimaliza, japo dakika za mwisho mambo yalikuwa mabaya”

“Unataka kuniambia kwamba serikali haifahamu kwamba wewe una kundi lako Al-quida?”

“Haifahamu kabisa, na wote wana amini kwamba mimi ni mwenzao”

“Una uhakika?”

“Asilimia mia moja. Mimi nipo serikali kama nilivyo kuambia pale awali, nina hitaji baadhi ya habari kutoka serikali, ndio maana unaweza kuona kikundi chetu hakiwezi kukamatwa kirahisi japo tuna fanya matukio makubwa sana duani”

“Hapa tutaondoka lini?”

“Kesho Alfajiri tutapanda ndege hadi Afghanistan”

“Mbona swala la safari hukuijulisha mapema?”

“Jamani mume wangu tumepata wapi muda wa kukaa chini mimi na wewe na kuzungumza juu ya kuondoka”

Farida alizungumza kwa sauti ya kudeka huku akinikumbatia. Akanipiga busu la mdomoni kisha akaondoka na kuanza kukagua nyumba yake alipo hakikisha kwamba ipo salama, tukavua nguo zetu na kuingia bafuni. Tukaanza kuoga taratibu, hisia za mapenzi zikatupanda na kujikuta tukianza kupapasana miili yetu, haukupita hata muda mwingi sana, tukajikuta tukizama katika penzi zito sana

***

Kama tulivyo panga asubuhi na mapema tukaanza safari ya kuelekea nchini Afghanistan. Ndege tuliyo ipanda abiria wengi ni waarabu na katika kuchunguza kwa haraka haraka, mtu mweusi ni mimi mwenyewe.

“Vipi mbona una jistukia?”

“Naona watu wote ni waarabu humu ndani kasoro mimi”

“Haahaa sasa hicho ndio kinakufanya ujistukie?”

“Ndio mke wangu?”

“Usijali”

Safari ya kutoka Saud Arabia hadi Afghanstan, ikatuchukua masaa wawili na dakika zake. Tukafika katika kiwanja kimoja kikubwa cha ndege, tukakodisha taksi ambayo moja kwa moja ikatupeleka hadi nje ya mji, ambapo tukakushuka katika eneo ambalo lina jangwa kidogo.

“Mbona tumeshUka jangwani sasa?”

“Tunapo kwenda huko haistahili dereva taksi kufika”

“Kwa hiyo tunatembea kwa miguu?”

“Ndio”

Nikashusha pumzi nyingi sana kwa maana huko tunapo kwenda ni jangwa tupu. Farida akaanza kutembea taratibu jambo lililo nifanya nianze kumfwata kwa nyuma. Ndani ya masaa mawili tunatembea kwenye jangwa hili lililo jaa mchanga mwingi huku machoni mwetu tukiwa tumevaa miwani kubwa za kuzuia mchanga.

“Aisee nimechoka?”

“Jikaze mume wangu”

“Farida tunakwenda wapi, mbele sioni tunapo kwenda zaidi ya mchanga tu, na nyuma sioni chochote mbona hivyo jamani”

“Sasa kama wewe mwanaume umechoka hivyo je mimi mwanamke ehee. Jikaze bwana”

Farida alizungumza huku akiendelea kutembea.

“Hili jangwa kwanza lina itwaje?”

“Rigestan huku ndipo yalipo makazi ya kikundi chetu japo pia kuna vikosi vya Wamarekani, wakiendelea kupitisha oparesheni ili kuweza kujua ni wapi kilipo kikosi chetu cha Al-Quida”

“Mmmmm”

“Naomba maji”

Farida akanikabidhi chupa kubwa ya maji tuliyo inunua kipindi tulipo kuwa tunatoka uwanja wa ndege. Tukazidi kusonga mbele huku Farida akiendelea kunisimulia mikasa mingi katika hili jangwa. Kwa mbali tukaona nyumba ndogo za undogo zikiwa zimejipanga vizuri.

“Tunyooshe mikono juu”

“Kwa nini?”

“Hiyo ni moja ya ishara ambayo inaweza kuwajulisha wezetu kwamba sisi ni wezao, endapo ukitembea kawaida unaweza kuuwawa kwa kudunguli kabal hata ya kufika katika zile nyumba na pia ukitembea hatua kadhaa hapo mbele kuna mionzi mikali ambayo usipo zimwa ni lazima ikuue kwa kukuta viande vinne”

“Duuu”

“Yaa hapa sasa ndio tunaingia kwenye kundi la Al-quida, hakikisha kwamba una kuwa nasi miaka yote, huku watu huifwata amri yangu ila endapo ukikiuka sheria na masharti ni lazima watakuua tu”

“Sawa mke wangu”

Tukatembea hatua chache, tukasimama mara baada ya kuona gari mbili aina ya pic up zikiwa zimejaa wanajeshi zikija katika eneo hili. Magari haya yakatuzunguka na wana jeshi wote wa kikosi hichi cha Al-quida wakashuka kwenye gari hili huku wakiwa wameshika mitutu mikubwa ya bunduki. Akashuka mzee mmoja mwenye ndefu nyingi huku sura yake ikiwa imeharibika vibaya na mkono wake mmoja ukiwa umekatika. Farida akapiga magoti chini na kuishika miguu ya mwanaume huyu huku akilia.

“Babaaaa”

Maneno ya farida yakanifanya niiishiwe na nguvu, kwani hadi sasa hivi bado sielewi ukweli wa maisha yake kwa maana kwa kumbukumbu zangu vizuri nina kumbuka alisha niambia kwamba baba yake alisha uwawa na wanajeshi wa Marekani na yeye ndio kiongozi wa kukindi hichi cha Al-quida, ina kuwaje baba yake yupo hai na ana mpigia magoti huku akilia.



Mzee huyo kwa kutumia mkono wake mmoja akamnyanyua Farida na kumkumbatia kwa nguvu.

“Baba nisamehe bado sijafikia kwenye malengo ambayo ulihitaji mwanao nifikie”

“Usijali nipo hapa kwa ajilia yako mwanangu ingieni kwenye gari”

Farida na baba yake wakaingia ndani ya gari huku mimi na wanajeshi wengine tukipanda nyuma ya gari hizi aina ya pick up. Magari haya yakageuzwa kwa kasi na kurudi katika ngome hii iliyopo hapa jangwani. Sio ngome kubwa kwa wingi wa majengo yake ambayo yametengenezwa kwa udongo. Gari zikasimama na tukashuka, kwa ishara Farida akaniomba niweze kufwatana nao, tukaingia kwenye moja ya nyumba kisha tukaanza kushuka kwenye ngazi zilizo elekea ardhini. Eneo la chini katika nyumba hii kuna kordo kubwa yenye taa kadhaa. Hapa ndipo nikagundua kwamba kambi hii ipo chini ya ardhi na huku chini ya ardhi kuna wanajeshi wengi wa kundi hili la Al-quida.

“Pole sana mwanangu”

“Asante baba”

Tukakaa katika kapeti zuri na lenye vijimito vidogo vidogo. Mzee huyu akanitazama kwa kunikazia macho usoni mwake.

“Kijana huyu umemtoa wapi?”

“Afrika, yeye ni Mnigeria, ila nilikutana naye Niger aliokotwa na mwanaume niliye kuwa nina ishi naye”

“Ahaa kijana unaitwa nani?”

“Randy”

“Baba, sisi na Randy adui yetu ni mmoja hivyo basi kuna mambo mengi ya kuweza kushirikiana naye”

“Kijana nakuomba uweze kutoka nje”

Mzee huyu alizungumza kwa sauti ya kukwaruza kidogo, nikanyanyuka na kutoka nje huku nikimtazama Farida usoni mwake. Nikasimama nje ya chumba hichi huku nikiwa nimejawa na wasiwasi mwingi sana. Mazungumzo ya Farida na baba yake yakachukua kama nusu saa, nikaona vijana wawili wakiingia ndani ya chumba hicho wakiwa na bunduki. Mara baada ya muda kidogo wakatoka, wakanishika kwenye mabega yangu kwa nguvu kama vile mwizi anavyo nyakuliwa na askari wa kutuliza ghasia.

“Munanipelekea wapi?”

Nilizungumza huku nikijaribu kujitoa mikononi mwao, ila sikuweza kuwazidi nguvu. Nikaanza kumuita Farida huku nikijaribu kujitoa mikononi mwao. Nikamuona Farida akiwa amesimama nje ya mlango wa chumba alicho kuwepo na baba yake huku machozi yakimwagika usoni mwake. Hapa nikatambua kabisa kwamba hali sio salama kwa upande wangu. Nikaingizwa kwenye moja ya chumba ambacho kimejaa damu damu kwenye sakafu na kwenye kuta zake. Nikakalishwa kwenye moja ya kiti cha chumba ambacho katika sehemu ya kikalio kuna duara moja kubwa sana ambalo ukikalia makalio lazima yatokeze kwa chini kidogo. Wanaume hawa wakanifunga kwa kamba ya manila kwenye mikono yangu pamoja na miguu yangu na kukosa namna ya kufanya. Wakaanza kuichana kanzu yangu kwa kutumia mkasi na nikabakiwa na boksa tu.

Mmoja wa vijana hao akachukua maji ya baridi yaliyomo kwenye ndoo kubwa na kunimwagia mwilini mwangu. Kijana mwengine akachukua mkasi na kuichana boksa yangu na nikabaki kama nilivyo zaliwa. Wakachukua vifaa viwili vilivyo unganishwa na nyaya za umeme, wakavigusanisha na kusababisha vitoe cheche kidogo.

‘Mungu wangu ni nini hichi?’

Nilizungumza huku nikiwa nimejawa na wasi wasi mwingi sana. Mwanaume huyu aliye zishika vifaa hivi akanigusisha navyo kifuani mwangu. Mtetemesho nilio upata mwilini mwangu, haki ya Mungu sikuwahi kuupata toka kuzaliwa kwangu. Si ngozi wala utumbo ambavyo vimeacha kutetemeka. Ukelele mkubwa nilio upiga haukusaida kumzuia mwanaume huyu kuendelea kunigusisha na vifaa hivyo.

“Ni nani aliye kutuma?”

Mwanaume huyu aliniuliza kwa sauti ya ukali sana swali ambalo sina jibu lake.

“Sina aliye nituma mimi”

Nilizungumza huku nikimwagikwa na machozi usoni mwangu. Mwanaume huyu akavigandamiza tena vifaa hivyo kifuani mwangu, nikazidi kuchanganyikiwa. Swali la mwanaume huyu ni moja tu, anahitaji kufahamu ni nani aliye nituma ila nami jibu langu ni moja kwamba hakuna aliye nituma. Mwanaume huyu alipo ona kwamba hakuna muafaka akavirudisha vifaa hivyo juu ya meza na mwenzake akachukua kamba moja kubwa ambayo mbele imefungwa fundo moja kubwa kiasi. Akalizungusha zungusha huku akinitazama usoni mwangu kwa tabasamu pana. Kwa nguvu zake zote akanipiga na fundo hilo la kamba chini ya kiti, na moja kwa moja likanipiga katika makend** yangu na kusababisha maumivu mara mia moja na maumivu ya shoti ya umeme nilio pigwa. Mishipa ya mwili niliishuhudia ikisimama na nikahisi muda wowote inaweza kupasua ngozi yangu na kunitoka.

“Ni nani aliye kuagiza kuwa na mahusiano na Farida?”

“Hakuna, nina mpenda tu”

“Muongo”

Mwanaume huyu akarudia kunipiga na fundo hilo la kamba na kunifanya nigugumie kwa uchungu mkubwa sana huku nikiwa nimeyang’ata meno yangu kwa nguvu sana. Mlango ukafunguliwa na akaingia baba Farida.

“Amesema chochote?”

“Hapana mkuu”

“Badilisheni zoezi”

Mzee huyu alisimama huku akinitazama kwa macho makali, nikafunguliwa kamba hizi na kulazwa chali chini, wakaingia vijana wengine wawili huku wakiwa wamejazia miilia yao. Wakanishika mikono yangu na kuitanua mithili ya Yesu alivyo kuwa akisulubiwa msalabani. Nikawekewa kitambaa kizito usoni mwangu, baada ya sekunde kadhaa nikaanza kuona maji mfululizo yakiingia mdomoni mwangu na puani. Nikaanza kufurukuta kwa kujitahidi kujitoa mikoni mwa wanaume hawa ila nikashindwa kabisa. Wakanifunua kitambaa hiki na nikaanza kuyatema maji haya huku nikiwa nimetokwa na jicho mithili ya mtu anaye iaga dunia kwa kujinyonga.

“Kwa nini umetembea na binti yangu?”

Nikashindwa hata kumjibu mzee huyu zaidi ya kumtazama usoni mwake.

“Endelea”

Mzee huyu alizungumza na zoezi likaendelea la kumwagiwa maji haya mengi. Mateso haya yakadumu kama nusu saa kisha wakanirudisha tena kwenye kiti na kuanza kunifunga kamba.

“Usipo sema ni nani aliye kuagiza kuwa na mahusiano na mwanangu ni lazima nitakuua umenielewa kijana?”

“Mze…ee…mimi sina mahusiano na binti yako. Una nionea tu”

Nilizungumza huku machozi yakinimwagika.

“Muacheni”

Mzee huyu alizungumza huku akitoka katika chumba hichi, vijana wake mara baada ya kumaliza kunifunga kamba wakatoka ndani humu na kuniacha mimi peke yangu. Nafsini mwangu nikajutia ni kwa nini nimemfahamu Farida na ni kwa nini nimekubali kuja katika kambi ya mateso kama hii, nilihisi kwamba nikija huku nitapata furaha na amani moyoni mwangu, ila kumbe nimekuja kukutana na shida na mateso mengi kama haya. Masaa yakazidi kuyoyoma nikiwa peke yangu ndani ya chumba hichi. Mwili wangu umetawaliwa na maumivu kila kona, nikaanza kukichunguza chumba hichi taratibu, japo hata kugeuza shingo yangu kutoka upande mmoja kwenda mwengine ni shuhuli sana. Kwenye moja ya kona katika hichi chumba kwa juu kuna kamera inayo rekodi matukio yote katika eneo hili.

Baada ya masaa kama mawili hivi toka niingizwe ndani ya hichi chumba, mlango ukafunguliwa na akaingia Farida akiwa amevalia nguo za kijeshi huku nyuma yake akiwa na walinzi wawili wa kike ambao nao pia wamevalia nguo za kujeshi.

“Mke wangu ni nini kinacho endelea?”

Farida hukunijibu zaidi ya kunitazama tu kwa macho yahuruma.

“Mke wangu niambie basi ni nini hichi kinacho endelea?”

Nilizungumza kwa ukali sana huku nikimtazama Farida usoni mwake, Farida machozi yakaanza kumwagika usoni mwake tu na akakosa jibu la kuzungumza.

“Kwa hiyo umenileta huku kuniua si ndio?”

Farida akageuka na kunipa mgongo, akaanza kutembea kuelekea nje.

“FARIDA, FARIDA, FARIDAAAAAAA”

Nilimuita Farida kwa nguvu sana ila hakuitika zaidi ya kuendelea kutoka nje ya chumba hichi na kuniacha mimi peke yangu. Uchungu na hasira vikatawala moyo wangu. Hakika Farida amenileta huku ili mradi aweze kunitesa. Mlango huu wa chumba ukafungwa kwa nguvu na nikabaki nikiendelea kulia.

‘Lazima nitoke humu ndani’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikitazama vifaa kadhaa vya mateso vilivyo pangwa kwenye meza kubwa iliyomo chumbani humu. Kama mwanaume ni lazima nitafute njia ya kujisaidia na sio kuendelea kupokea mateso kama haya ambayo siyaelewi kabisa chanzo chake ni nini. Nikaanza kujisogeza karibu na meza hii huku nikijaribu kijitahidi kutembea na vidole taratibu, ila katika harakati za kufika katika meza kwa bahati mbaya nikaangukika mbavu zangu za upande wa kushoto na nikashindwa kuendelea na jitihada zangu na nikaendelea kusikilizia maumivu makali ninayo yapata.

Siku nzima ikapita nikiwa katika hali ya maumivu. Masaa yakazidi kuyoyoma huku panya na mende wakakatiza katika katika eneo hili. Mlango ukafunguliwa na akaingia mwanaume aliye valia nguo nyeusi huku mkononi mwake akiwa ameshika roba jeupe.

“Furahia maisha ya usiku huu”

Mwanaume huyu akaliweka roba hilo chini kisha akatoka ndani, nikaanza kuona siafu wengi wakitoka ndani ya roba, siafu hawa kama vile wameelekezwa waje kwangu, kwa kasi wakaanza kunipandia mwilini mwagu na kuanza kuning’ata kisawa sawa. Ukijumlisha maumivu ya shoti ya umeme niliyo pigwa, maumivu ya kupigwa katika sehemu zangu za siri ukichanganya na maumivu haya ya siafu hakika nikaanza kuona roho yangu ikanza kunitoka. Nikalia hadi sauti yangu ikanikauka, hali ikazidi kuwa mbaya hadi ikafika hatua nikapoteza fahamu.

***

Taratibu nikafumbua macho yangu, nikaona mwanga hafifu wa taa, huku mbele yangu kukiwa na watu kama sita walio valia nguo za jeshi wakiwa wamesimama na mitutu yao ya bunduki. Wanaume hawa wote ni waarabu, nikajichunguza mwilini mwangu na kujikuta nikiwa nimevishwa nguo za jeshi huku mikono yangu ikiwa imefungwa pingu.

“Simama”

Mwanaume mmoja alizungumza, nikashusha pumzi taratibu, nikajikaza na kusimama huku nikiwa nina yumba yumba. Eneo hili tulilipo ni jangwani na kuna upepo mkali sana na vumbi jingi.

“Nipo wapi hapa?”

Niliwauliza wanaume hawa ila hakuna hata mmoja wao aliye weza kunijibu. Baada ya muda kidogo tukaanza kusikia mingurumo ya magari, tukaona gari tatu zikija kwa kasi, gari hizi zikasimama mita chache kutoka hapa tulipo. Wakashuka wanajeshi wengine wanne wakiwa na bundiki ambao nao pia asili yao ni waarabu. Mmoja wa wanajeshi aliyepo upande wetu akanishika mkono katika eneo la kwapani na tukatembea taratibu hadi kwa watu hawa walio kuja katika eneo hili.

“Yupo vizuri?”

Mwanajeshi mmoja aliuliza.

“Ndio”

Kwa ishara ya kichwa mwanajeshi huyu akamuomba mwenzake aniingize ndani ya gari. Nikaingizwa ndani ya gari la katikati na wanajeshi hawa wakaendelea kunzungumza kwa muda kidogo kisha, wakaingia kwenye gari na safari ya kuondoka hapa ikaanza. Wanajeshi hawa hawakunieleza chochote zaidi ya kuendelea na safari katika jangwa hili.

Tukafika kwenye moja ya kambi ya jeshi, nikashushwa na nikafunguliwa pingu zangu huku mwili mzima nikitembea kwa kutetemeka kutokana na maumivu makali sana ambayo niliyapata. Nikafunguliwa pingu za mikononi mwangu, kwa ishara huku nikiwa nimeshikiwa mtutu na mwanajeshi mmoja nikaamrishwa kutembea. Tukafika kwenye moja kikosi cha wanajeshi wanao tembea juu ya kamba, mkuu wa mafunzo hayo akanong’onezwa na mwanajeshi huyu kisha mwanajeshi huyu akaondoka huku akinitazama usoni mwangu.

“Panda kule”

Mwanajeshi huyu aliniambia kwa amri, nikaanza kujikokota kwani kila sehemu ya mwili wangu kusema kweli ina niuma sana. Nikafika katika eneo lililo ning’inizwa kamba ngumu, nikachukua moja na nikaanza kupanda kamba hii kwa maana tayari haya mafunzo nilisha wahi kuyafanya. Nikajitahidi kiume na nikafanikiwa kulimaliza tatizo hili.

Siku zikazidi kusonga mbele huku nikiwa nimesha zoea mafunzo katika kambi hii. Juhudi yangu katika mafunzo nayo taratibu ikaanza kunipatia nafasi ya kupendwa na waalimu hawa wa mafunzo. Mafunzo haya ya kijeshi yakatuigarimu zaidi ya miezi sita huku akilini mwangu nikiwa tayari nimesha mfuta Farida, kwa maana hana faida tena kwenye maisha yangu.

“Leo kuna kazi munapaswa kwenda kuifanya”

Mkuu wetu wa mafunzo katika kambi hii alizungumza huku tukiwa kwenye moja ya ukumbi wetu wa mikutano katika hii kambi. Ikawashwa projecter ikawashwa na kumulika ukutani.

“Leo makamu wa raisi wa nchi ya Marekani anakuja nchini hapa Afughanistan. Tunatakiwa kuhakikisha kwamba leo hii anaingia mikononi mwetu.”

Wanejeshi wote tukaa kimyana kuendelea kumsikiliza kwa umakini mkufunzi wetu.

“Watu wanao takiwa kwenda hapa ni watano. Lazima kuwe na wadunguaji wawili, wapambanaji watatu. Randy utaongoza kikoso kizima katika swala la upambanaji”

Nikastuka kidogo ila sikuhiji kuonyesha mstuko wangu kwani moja ya sheria katika jeshi ni lazima mtu ufwate amri ya mkuu wako pasipo kupinda. Wakachaguliwa wezangu watano na tukaelekea katika chumba cha maandalizi. Kila mmoja akachagua silaha ambayo anakwenda kuitumia katika kazi hii tuliyo pewa kwa kustukiza. Ni kazi moja nzito na ngumu sana kwa maana kila mmoja ana jua jinsi Wamarekani wanavyo kuwa makini kuimarisha ulinzi kwa viongozi wao hususani pale wana kuja katika nchi ambazo hazina amani kama hii Afghanstan. Akaingia mkufunzi wetu akiwa ameshika laptop mkononi mwake, akatuita kwa pamoja na tukamzunguka na akaanza kutupa maelezo ya nini ambacho tunapaswa kwenda kukifanya katika kazi hii.

“Hakikisheni kwamba munamleta hapa akiwa hai mumenielewa”

“Sawa mkuu”

“Kuna mwenye swali?”

“Ndio mkuu”

Mmoja wetu alizungumza na sote tukaa kimya kumsikiliza.

“Je ikitokea tukashindwa kumchukua akiwa hai na kwa bahati mbaya tukamuua itakuwaje mkuu?”

“Hii ni kazi ya kuteka na si kuua, ila kama kuna walinzi wake hakikisheni kwamba munawau”

“Sawa mkuu”

“Kuna angalizo munatakiwa kulifanya. Katika kazi hii kuna mtu huyu atajitokeza”

Mkuu akatuonyesha picha ya mwanaume mmoja kijana kabisa akiwa amevalia shati jeusi.

“Huyu ni gaidi wa dunia, hadi kesho bado haja patikana ana itwa DANY. Endapo mutacheza vibaya basi nina amini hakuna hata mmoja wenu anaye weza kurudi akiwa hai mume nielewa?”

Moyo wangu ukanistuka mara baada ya kumsikia adui aliye niulia baba yangu kwamba naye atakuwepo kwenye kazi hii na huku pia atakua ni adui yangu. Kwa mafunzo na uwezo nilio nao, nikajiapiza kimoyo moyo endapo Dany atajitokeza kwenye hili swala basi ama zake au ama zungu nilazima nitammaliza.



“Mkuu nina swali?”

“Uliza?”

“Huyu Dany atakuwepo kama nani, mtekaji, muuaji au muokoaji?”

Swali la mwezetu mmoja likatufanya tumtazame mwalimu usoni mwake.

“Hadi sasa hivi hatujajua lengo na dhumni lake yeye kuwepo hapo, ila huyu ni gaidi ambaye ana uhasama mkubwa sana na nchi ya Marekani, hivyo hatujajua kwamba atakuja au laa. Hivyo umakini wenu ni muhimu sana kwenye hii kazi”

“Sawa mkuu”

“Munatakiwa kuvaa suti nyeusi na kila mmoja vitakuwa na vitambulisho vinawaonyesha kwamba nyinyi ni wana usalama wa Marekani wanao mlinda raisi. Randy hakikisha unaongoza hichi kikosi vizuri sawa”

“Sawa”

“Usiku huu”

Kila mtu akaletewa suti yake nzuri pamoja na kitambulisho. Tukavaa na kukabidhiwa magari mawili meusi aina ya GMC ACADIA DENAL, ambayo leo ndio yanatumiwa na walinzi wa raisi wa Marekani. Nikawasha moja ya gari kisha taratibu tukaanza kuondoka kwenye kambi hii huku tukiifwata ramani inayo ongozwa na mfumo wa GPRS kueleeka katika mji wa KABUL ambapo kuna sherehe inayo fanyika usiku huu kwenye hoteli moja inaitwa Kabul Serena Hotel.

“Kila mmoja avae kinasa sauti, hii kazi ni lazima tuweze kuifanikisha leo hii”

Nilizungumza huku nikivaa kinasa sauti changu kwenye sikio. Safari ikatugarimu masaa mawili kufika katika mji wa Kabul. Tukafika katika hotel ya Kabul Serena, tukazisimamisha gari zetu mita kadhaa kabla ya kufika katika hoteli hiyo.

“Wawili watawanyike”

Wakashuka watu wanao husika na maswala ya udunguaji, kisha sisi tukaendeleana safari ya kuingia ndani ya hoteli hiyo. Tukaonyesha vitambulisho vyetu vikakaguliwa katika mashine maalumu, tukarudishiwa vitambulisho vyetu na tukaruhusiwa kuingia ndani ya hoteli hii ambayo tayari magari mengi ya wageni ambao wamekuja katika sherehe hii maalumu ya kuadhimisha kumbukumbu za kuzaliwa kwa raisi wa nchi hii na kwa bahati nzuri raisi wa Marekani ana ziara ya siku mbili katika katika nchi hii.

“Kila mmoja aweze kutawanyika, kumbukeni kwamba kazi iliyo tuleta hapa ni kuhakikisha kwamba tunaondoka na makamu wa raisi”

“Sawa mkuu”

Tukashuka kwenye kwenye magari na kutawanyika kila mtu sehemu yake huku kila mmtu akiwa makini kuhakikisha kwamba tunafanikiwa kumuona makamu wa raisi wa Marekani. Haukupita muda mrefu raisi wa nchi hii akatoka nje na watu wake kwenda kumpokea mgeni wake ambaye ni makamu wa raisi wa Marekani. Wakaingia kwenye ukumbi huu ambao ulinzi umeimarishwa vizuri. Kazi yangu na wezangu wawili ambao tumeingia nao ndani ya hoteli hii ni kuhakikisha kwamba tunawafahamu walinzi wote wa siri wanao mlinda makamu wa raisi kwani walinzi wanao mlinda raisi si wote ambao wamevalia suti.

“Kuna chohote mulicho kigundua”

“Hapana mkuu”

Vijana wangu walinijibu kila mmoja kwa wakati wake. Tukaendelea kuzunguka zunguka ndani ya ukumbi huu. Gafla taa zikazima na tukaanza kusikia milio ya risasi jamboa mbali sio ambalo lipo kwenye mpango wetu tulio upanga.

“Ni nini kinacho endelea?”

Niliwauliza vijana wangu ila hapakuwa na hata mmoja ambaye akiweza kunipatia jibu. Milio ya risasi na vilio vya watu vulizidi kuandama. Kitu kibaya ni kwamba sina hata miwani ambayo inaweza kuniwezesha kuona katika giza. Kwa bahati nzuri nikamuona makamu wa raisi akikimbizwa na walinzi wake kuelekea katika moja eneo ambalo kwao naamini kwamba ni eneo salama. Nikaanza kuwakimbiza kwa nyuma huku nami jukumu langu ni kuhakikisha kwamba ninampata raisi.

Kwa bahati nzuri nikawafikia na tukaingia sote kwenye lifti huku wakiamini kwamba mimi ni wakwao.

“Ni nini kinacho endelea?”

Makamu wa raisi aliuliza kwa wasiwasi mwingi sana.

“Hatujafahamu mkuu hata wezetu nje hakuna ambaye anatupa ripoti”

Mlinzi mmoja alizungumza huku akihema sana. Lifti ikaanza kupanda kwenda juu huku sote tukiwa na wasiwasi mwingi sana. Tukafika gorofa ya tano lifti ikafunguka na wakatoka walinzi wawili huku wakiwa makini sana.

“Clear”

Walizungumza huku wakimaanisha kwamba kuna usalama. Tukamtoa makamu wa raisi huku tukitembea kwenye kordo hii kwa umakini sana. Tukaingia kwenye moja ya chumba, walinzi walio tangulia wakakagua usalama, kisha tukaingia ndani huku tukiwa tumemuweka makamu wa raisi katikati yetu. Walinzi wa Marekani wapo watano huku nami nikiwa ni mtu wa sita.

Kila mlinzi yupo makini katika kuhakikisha kwamba makamu wa raisi yupo salama. Gafla akaanguka mlinzi mmoja huku risasi ikitokea kwenye dirisha moja la kioo. Shambulizi hili likazidi kutuchanganya. Kwa haraka haraka nikakumbuka kuhusiana na uwepo wa Dany katika swala hili. Risasi mufululizo zikaanza kuingia kutokea mlangoni na kunifanya na mimi nianze kujibu mashambulizi hayo.

Kusema kweli usiombee kufanya mashambulizi na watu ambao hujui wapo wapi, kwani kila muda unavyo zidi kwenda ndiyo kila jinsi walinzi wa makamu wa raisi wanavyo teketea. Tukabaki mimi na makamu wa raisi huku risasi zikiwa zimeniishia kwenye magazine.

Mlango ukaanguka wote na nikamshuhudia mwanaume aliye valia nguo nyeusi tupu na uficha sura yake akiwa amesimama huku mkononi mwake akiwa ameshika mtutu mkubwa wa bunduki. Taratibu nikashusha pumzi huku nikimtazama makamu wa raisi jinsi anavyo tetemeka mwili mzima.

Mwanaume huyu akanitazama kwa muda huku akianza kupiga hatua za kuingia humu ndani. Mwanaume huyu akatupa bunduki yake chini huku akizidi kutembea kwa kujiamini akitufwata sehemu tulipo simama na makamu wa raisi.

Kama mwenajeshi niliye kamilika katika mafunzo moja ya sheria ni kuto kufa kibudu ni bora uhakikishe kwamba una pambana hadi kufa. Kwa haraka nikalivua koti langu la suti huku nikimtazama mwanaume huyu. Nikaanza kurusha mateke, ila kila teke ninalo lirusha mwanaume huyu analikwepa. Nikajaribu kurusha ngumi kadhaa, ila nikashindwa kabisa kumgusa hata mwili wake kwani ni mtu mmoja mwepesi ambaye anawesza kukataa kila shambulizi analo pelekewa. Akanipiga teka moja la kifua na kunifanya nianguke chini huku nikihema sana. Kwa ishara akaniomba nisimame, nikajithaidi na kujipanga tena, nikaendelea kuhakikisha kwamba ninamshambulia, ila nilicho ambalia ni kupigwa kisasa sawa huku makamu wa raisi akiwa ameendelea kujikunyata na ujanja wote wote umemuishia.

“Nenda kawaambie waalimu wako wakufundishe tena kijana na usirudie kuifanya hii kazi tena”

Maneno ya mwanaume huyu yakazidi kunipa hasira, kwani mafunzo yote niliyo yapata kwa kipindi cha miezi zita si kitu mbele yake, kwani sijafanikiwa kumpiga ngumi hata moja. Mwanaume huyu akachomoa bastola nyingine na kumpiga makamu wa raisi, ila haikutoka risasi zaidi kisindano kilicho mfanya makamu wa raisi kulegea na mwishowe akalala usingizi fofofo. Nikamshuhudia akimnyanyua makamu wa raisi na kumuweka begani mwake, akaanza kutembea naye kuelekea mlangoni.

“Heii wewe ndio Dany?”

Niliuliza kwa kujikazana na mwaume huyu akasimama, kisha taratibu akanigeukia na kunitazama sana, taratibu akavua kitambaa kilicho ificha sura yake. Moyo ukanistuka, hasira ikazidi kunipanda, kwani ni Dany mwenyewe.

“Pumbavu wewe umeniulia baba yangu”

Nilizungumza kwa hasira huku nikiksimama kwa kujikaza, nikaanza kumkimbilia katika sehemu alipo simama, kabla sijamfikia akanipiga risasi ya sindano kwenye paja langu, nikajitahidi kutembea ila kadri sekunde zinavyo zidi kwenda ndivyo jinsi mwili wangu ulivyo zidi kunilegea na mwisho nikajikuta nikianguka chini kabisa.

“Muambie aliye kueleza historia hii, akueleweshe vizuri nani ni baba yako sawa na kama ukishindwa nenda Tanzania utajua ukweli”

Taratibu Dany akavaa kitambaa chake na kutoka ndani humu na kuniacha nikipitiwa na usingizi na mwisho nikalala usingizi fofofo.

***

Kelele za watu wanao zungumza zikanifanya nifumbue macho yangu. Nikaona madaktari na waokoaji wengine wakizunguka zunguka ndani ya chumba hichi.

“Hei”

Daktari mmoja wa kike alizungumza huku akininamia.

“Mmm”

“Unasikikiaje?”

Nilizungumza huku nikinyanyika, nikatazama ndani humu na kuona jinsi miiili ya walinzi wengine jisni ilivyo zagaa kwa kupigwa rasasi. Nikaichomoa sindano hii iliyo nichoma kwenye paja langu kisha taratibu nikasimama huku daktari huyu akinisaidia nisianguke.

“Unajisikiaje?”

“Nahitaji kuondoka hapa”

Nilizungumza huku nikijihisi kizungu zungu kikali sana.

“Inabidi upate huduma ya kwanza”

“Nahitaji kuondoka nisindikize hadi kwenye maegesho ya magari”

Nesi huyu mwenye asili ya kiarabu akanitazama kwa sekunde kadhaa kisha akanishika mkono na kiuno changu na taratibu tukaanza kutoka katika chumba hichi huku mwilini mwangu nikihisi maumivu makali. Nikaanza kujisunya mimi mwenyewe huku nikiwa ni jazba, kwanza ya kupigwa pili ya kushindwa kukanilisha kazi iliyo nileta na tati sijafamu ni kwa nini Dany aliniambia kwamba aliye nieleza juu ya kuuwawa kwa baba yangu, anatakiwa kunieleza vizuri la sivyo nielekee nchini Tanzania.

“Mbona una jisunya hivyo?”

Nikamtazama nesi huyu huku nikiendelea kujisunya, sikumjibu kitu cha ina yoyote. Tukafika eneo la maegesho ya magari huku kukiwa ni majira ya saa kumi na moja asubuhi. Ulinzi katika hoteli hii umezidi kuimarishwa na kuna vikosi mbalimbali vya usalama vipo hapa kuhakikisha kwamba kila jambo linakwenda vizuri.

“Gari lile pale”

Nilizungumza huku nikinyooshea gari moja wapo kati ya magari tuliyo kuja nayo. Nesi akanifikisha katika gari hilo.

“Unaweza kuendesha kweli kwa hali yako ume umia sana”

Nesi huyu alizungumza huku akinitazama usoni mwake. Nikatazama jinsi watu wanavyo kaguliwa katika geti la kutokea katika hoteli hii.

“Niendeshe?”

“Nipo kazini”

“Naomba uniendeshe?”

Nilizungumza kwa ukali sana huku nikimtazama nesi huyu. Nesi huyu taratibu akafungua mlango gari hili upande wa dereva na kuingia ndani. Nami nikaingia ndani ya gari hili na taratibu tukaanza kuondoka katika eneo hili. Tukafika getini na tukakaguliwa, tukaruhusiwa kuondoka katika eneo hili.

“Nahitaji msaada wako”

“Msaada wangu wa nini?”

“Kiafya”

“Inabidi tukupelekea hospitalini?”

“Sihitaji kuelekea hospitalini naomba unisaidie sehemu yoyote tofauti na hospitalini”

“Kwa nini?”

“Nahitaji nifanye kazi ya kumkomboa makamu wangu wa raisi”

Nesi huyu akanitazama kwa mshangao.

“Wewe ni Mmarekani?”

“Ndio”

“Pole sana kwa kilicho tokea”

“Asante”

“Nitakupeleka nyumbani kwangu kukupatia huduma”

“Sawa”

Tukafika katika mtaa wenye nyumba nyingi nyingi zilizo jipanga vizuri. Tukashuka kwenye gari, nikalitazama eneo hili viruzi kisha nikazunguka nyuma ya gari hili, nikafungua mlango wa nyuma wa hili gari, nikatoa bastola moja na kutoa magazine mbili zilizo jaa risasi kisha nikafunga. Tukaingia ndani ya nyumba ya nesi huu huku nikichechemea mguu wangu ambao ulipigwa risasi iliyo kaa mfumo wa sindano.

“Unaishi na nani?”

“Peke yangu”

Nesi huyu alizungumza huku akifungua mlango, tukaingia ndani ya nyumba hii, nikaanza kuikagua eneo zima la ndani kisha nikarudi sebleni, nikamkuta nesi akiwa tayari amesha andaa vifaa vyake vya kunihudumia.

“Unaitwa nani?”

Nesi aliniuliza huku akivaa gloves nyingine hii ni mara baada kuvua gloves alizo kuwa amezivaa kwenye viganja vyake.

“Randy”

“Ilikuwaje hadi hoteli ikavamiwa?”

“Siwezi kukujibu swali hilo kwani wewe sio mkuu wangu wa kazi”

Nesi akanivua shati langu ambalo limechafuka kwa kiasi kisha akaanza kunipaka dawa ya maji kwenye sehemu nilizo pigwa kipigo na Dany ambaye kwa kweli amezidi kunipa hasira ya kuhakikisha kwamba nilazima nitamuangamiza tu.

“Hii dawa yake kazi yake ni nini?”

“Kufuta maumivu”

“Ahaaa……..sawa sawa”

Nesi akamaliza matibabu yake.

“Ninakwenda kukuandalia kifungua kinywa”

“Hapana sihitaji kunywa sasa hivi, asante kwa msaada wako”

Nilizungumza huku nikisimama. Nikavaa shati langu na kuanza kuelekea nje.

“Unakwenda wapi?”

“Kuna kazi ninahitaji kuhifanya na sina muda wa kuendelea kuwepo hapa samahani kama nitakuwa nimekuudhi”

Nilizungumza huku nikielekea nje, kitendo cha kufungua mlango nikastukia nikirudishwa ndani kwa nguvu mara baada ya gari langu kulipuka kutokana na bomu ambalo lilitegwa kwenye gari pasipo mimi mwenyewe kutambua.



“Fuc** meee”

Nilizungumza huku nikishuhudia moshi mwingi unavyo ambaa ambaa katika eneo hili huku moshi mwengine ukiingia ndani humu. Taratibu nikaanza kunyanyuka huku nikiyumba yumba. Nikamuona nesi akiwa ameanguka chini, kwa haraka nikamsogelea na kumnyanyua, nikamkimbiza chumbani kwake na kumlaza kitandani, nikaanza kumpa huduma ya kwanza ya kufungua vifungo vya koti lake alilo livaa. Nikamfungua vifungo vya shati lake na kumuacha na sidiria. Maziwa yaliyo simama vizuri ya nesi huyu yakanifanya nishikwe na bumbuwazi kiasi. Nikiwa katika hali ya mshangao, nikahisi kuna watu wanaingia ndani ya nyumba hii, kwa haraka nikachomoa bastola yangu vizuri na kutoka nje kwa umakini. Nikawaona watu walio ficha sura zao, wakiingia huku wakiwa wameshika mitutu ya bunduki, mmoja wao kwa bahati akaniona.

“Yule kule”

Aliwambia wezake huku akianza kufyatua risasi ambazo sikuweza kufahamu ni kikosi gani cha watu ambao wamepanga kunishambulia. Nikakimbilia chumbani alipo nesi huyu na kumkuta akiwa amekaa kitandani huku akiwa amejawa na mshangao.

“Kaaa pembeni kule”

Nilizungumza kwa ukali na nesi huyu akaweza kunielewa, kwa haraka akaingia bafuni. Mlango wa chumba hichi ukazidi kushambuliwa kwa risasi.

“Njoo huku”

Nesi alizungumza na kunifanya niingie bafuni humu, akafunga mlango. Akazogeza kioo kidogo kilichopo humu ndani, nikaona kitasa. Akafungua mlango huu ambao unafanania na ukuta wa humu ndani, tukatokea eneo la uwani katika nyumba hii. Nesi huyu akaanza kujifunga vifungo vya shati lake.

“Ni kina nani wale?”

Nilimuuliza nesi huyu huku nikichungulia katika eneo la mbele katika nyumba hii na nikaona gari mbili aina ya pick up zikiwa zimesimamishwa.

“Hichi ni kikosi cha ISS”

“Ndio kina nani?”

“Hawa ni wafuasi wanao pingana na Wamarekani. Hivyo wamekuja hapa kwa lengo la kukuchukua wewe na isitoshe wameweza kuona gari hio ya Kimarekani hapa”

Nesi alizungumza huku jasho likimwagika usoni mwake.

“Fuc** me”

Nilizungumza huku nikiishika vizuri bastola yangu.

“Nisubirie hapa sawa”

Nesi akanijibu kwa kutingisha kichwa, nikaanza kunyata huku nikielekea katika eneo zilipo gari hili, nikawaona wapiganaji wawili wakiwa wamesimama huku wameshika mitutu mikubwa ya bunduki. Sikutaka kuwapa nafasi ya kufanya jambo lolote kwangu, nikaanza kuwashambulia mmoja baada ya mwengine. Milio ya risasi iliweza kuwastua wezao walipo ndani, kwa haraka nikakimbilia kwenye moja ya gari na kujibanza sehemu ambayo hata wakishambulia kwa risasi hawato weza kunipata. Mashambulizi kati yangu na wao yalizidi kupamba moto, kwani wapo ndani na ni rahisi kujificha na kushindwa kupatwa na risasi.

“Weka silaha yako chini”

Nilisikia sauti ya ukali kutoka kwa mmoja wa wapiganaji. Nikachungulia na kumuona wakiwa wamemshikilia nesi aliye nisaidia.

“Moja…..Mbili”

Kabla hajafikisha tatu, nikajitokeza katika sehemu nilipo jificha huku nikiwa nimeinyoosha mikono yangu juu. Nikaitupa bastola yangu pembeni, ikiwa ni ishara ya kujisalimisha kwao ili mradi niweze kuyaokoa maisha ya nesi huyu. Wakanifwata wapiganaji wawili, wakanipiga na kitako cha bunduki kwenye paji langu la uso, nikaanguka chini mzima mzima huku nikiona maruwe ruwe. Wakaniongezea na teke zito la kichwa ambalo likanipelekea kupoteza fahamu kabisa.

***

Harufu kali ya kinyesi iakaanza kupenya puani mwangu. Taratibu nikafumbua macho yangu. Eneo nililopo ni ndani ya kisima cha kinyesi huku mikono yangu ikiwa imefungwa kwa kamba juu ya bomba kubwa la chumba huku nusu ya mwili wangu, ikiwa ndani ya kisima hichi cha kinyesi. Kambi hii ni toafauti sana na kambi ya kikosi cha Al-quida ambacho ndipo ninapo fanyia kazi. Kambi hii moja kwa moja inaonyesha kwamba ipo porini, kwani imezungukwa na miti mingi sana. Nikaona kundi kubwa la wanajeshi wakija katika eneo nilipo mimi. Walipo fika, wanajeshi wawili wakaanza kuivuta kamba hii na taratibu mwili wangu ukaanza kutoka katika kisima hichi cha kinyesi.

“Mtoeni”

Mzee mmoja aliye valia kanzu na koti la jeshi huku kichwani mwake akiwa amejifunga kilemba cheupe alizungumza, taratibu wakanitoa huku nusu ya mwili wangu ikiwa imejaa kinyesi na nipo uchi kama nilivyo zaliwa. Kwa ishara akawaamrisha vijana wake kuanza kunikokota kwa kuniburuza hadi tukaingia kwenye moja ya kibanda. Nikakalishwa kwenye kiti cha chumba hichi, kisha nikafungwa kamba mwili mzima huku nikiendelea kunuka kinyesi.

“American soujar, ni nini kilicho kuleta hapa Afghanistan?”

Mzee huyu alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.

“Mimi sio Mmarekani”

Maneno haya yakamfanya mzee huyu kutabasamu kisha akacheka kicheko cha dharau sana.

“Kama sio Mmarekani, wewe ni nani?”

Nikaa kimya huku nikimtazama mzee huyu kwa umakini sana.

“Kamleteni”

Mzee huyu alitoa amri, wakatoka vijana wawili, baada ya muda kidogo wakarudi wakiwa wameongozana na nesi waliye mteka. Nesi akastuka sana kuniona nikiwa katika hali kama hii.

“Usipo zungumza ukweli, malaya wako ana kufa”

Mzee huyu alizungumza huku kijana wake mmoja akiwa amemuwekea bastola ya kichwa nesi huyu.

“Wewe ni ni nani?”

“Mimi ninaitwa Randy. Ni mpiganaji wa kikundi cha Al-quida, nilikuja hapa kwa kazi moja tu, kuhakikisha kwamba ninamteka makamu wa raisi wa Marekani, ila mission yangu iliingiliwa na gaidi mmoja anaye itwa Dany aliwaua wezangu wote na pamoja na walinzi wa Marekani na akaondoka na makamu wa raisi”

Mzee huyu akaka kimya kwa sekunde kadhaa.

“Nitajie jina la mkuu wako wa Al-Quida?”

“Farida ama Hawa ni mjukuu wa musisi wa Al-quida, mzee Osama Bin Laden”

Mzee huyu akakaa kimya kwa muda huku akinitazama usoni mwangu.

“Mkuu wako wa Al-quida anaitwa nani?”

“Saad bin Laden”

“Mpelekeni kifungoni”

Vijana wake wakanifungua kamba walizo nifunga kwenye kiti hichi, wakanitoa nje ya kibanda hichi na wakainiingiza kwenye moja ya chumba chenye dirisha dogo kwa juu huku mlango wake ukiwa ni wa chuma.

‘Fuc**”

Nilizungumza huku nikikaa chini, harufu kali inayo toka mwilini mwangu hakika hata mimi mwenyewe inanikosesha amani kiasi cha kujikuta nikijichukia mimi mwenyewe. Mlango ukafunguliwa na akaingia nesi huyu huku akilia.

“Hei hei. Kila kitu kitakuwa sawa”

Nilijiaribu kumbeleza huku nikijaribu kumshika, ila nilivyo jigundua kwamba ninanuka nikaurudisha mkono wangu.

“Kwa nini nilikusaidia khaaa?”

Nesi alizungumza huku akimwagikwa na machozi.

“Usijali kila jambo litakuwa sawa, hawawezi kutuua, sawa nesi”

Nesi akanitazama kwa macho ya ukali sana kisha akaachia mfyonyo mkali sana kisha akakaa kwenye moja ya kona huku akiwa ameziba pua yake.

“Kwa nini umekuwa ni muongo kwangu?”

Muongo kivipi?”

“Kumbe wewe ni Al-quida, alafu ukaniambia ni Mmarekani”

“Unahisi kila jambo ni rahisi kumuamini mtu au?”

“Hata kama ungeniambia tu”

“Nisikilize, nimejisalimisha maisha yangu kwa ajili yako, pale sikushindwa kuwatoroka wale wanajeshi, ila nilijitahidi kuwa mpole kwa ajili yako, ila unaona msaada wangu ni wakijinga si ndio?”

Nilizungumza kwa ukali kidogo hadi nikamuona nesi akitetemeka mwili wake.

“Muda huu sio wakutupiana lawama. Ni muda wakujua ni nini tunafanya”

Taratibu nikasimama na kutembea hadi ulipo mlango, nikaanza kugonga kwa nguvu. Mlango ukafunguliwa na wakasimama vijana wawili wakiwa wameshika mitutu ya bunduki.

“Hata kama mumenishikilia, ninahitaji munisafishe mwili wangu”

Nilizungumza kwa ukali, mlango ukafungwa na vijana hawa pasipo kunisemesha kitu chohote. Nikaupiga mateke huku nikiwatukana matusi ya kila aina.

“Hei, hei”

Nesi alizungumza huku akinisogelea. Taratibu akavua koti lake na kunikabidhi.

“Vaaa”

“Nitavaaje nikiwa na kinyesi?”

“Vaa ujisitiri sio vizuri kwa mimi mwanamke ambaye sio mke wako, nikaona maungo yako”

Nesi alizungumza kwa upole na ukarimu mkubwa sana hadi mimi mwenyewe nikastukia.

“Samahani, ila siwezi kuchafua koti lako, wewe endelea kuvumilia kuona maungo yangu”

Nilizugumza huku nikirudi kukaa kwenye eneo nililo kuwa nimekaa.

“Unaitwa nani?”

Nilimuuliza nesi huku nikimtazama usoni mwake.

“Husna”

“Ahaa una jina zuri”

“Asante”

“Ume olewa?”

“Hapana”

“Kwa nini sasa?”

“Muda wangu ukifika nitaolewa”

“Sawa”

“Kwa nini ulijiunga na Al-quida?”

“Ni stori ndefu sana”

Ndani ya muda mfupi mimi na huyu nesi tukajikuta tukiwa ni marafiki, akaanza kunisimulia historia ya maisha yake, toka alipo kuwa binti mdogo. Tukiwa katikati ya mazungumzo, mlango ukafunguliwa kwa ishara nikaitwa na mwanajeshi mmoja.

“Ninakuja”

“Sawa”

Nesi alizungumza huku akiwa amejawa na tabasamu pana. Nikafungwa pingu za mikononi, kutokana nipo chini ya ulinzi mkali, sikuhitaji kuleta ubishi wa aina yoyote. Tukaingia kwenye moja ya bafu, wakaanza kunimwagia maji mwilini mwangu kwa kutumia mpira wa maji yanayotoka kwa nguvu sana. Kusema kweli maji haya yanaumiza mwili, ila sikuwa na namna ya kufanya. Baada ya kinyesi chote kuondoka mwilini mwangu, wakaanza kunifungua pingu kisha wakanikabidhi sabuni kwa ajili ya kuoga mimi mwenyewe.

“Una dakika tano za kuoga”

Mwanajeshi huyu alizungumza huku akisogea hatua kadhaa kutoka katika sehemu nilipo simama. Nikaanza kuoga taratibu huku nikiwatazama kwa umakini. Nilipo maliza tukaondoka katika eneo hili na tukingia kwenye moja ya ofisi na nikawakuta wanajeshi wenzangu watatu wa kundi la Al-quida, wakizungumza na mkuu wa kikundi hichi.

“Una bahati kijana, nimeweza kuletewa taarifa zako sahihi”

“Ulihisi nina kudanganya mzee wangu?”

“Mimi sio mtu rahisi wa kuamini watu, ila kwako nimeweza kukuamini, ndio maana ninakuambia kwamba una bahati”

“Asante mzee”

Nikakabidhiwa nguo za kijeshi mbazo wamekuja nazo hawa wezangu. Makubaliano ya kukabidhiwa kwa wanajeshi wezangu yakasainiwa kwenye karatasi fulani kisha tukatoka nje na kuelekea kwenye eneo la magesho ya magari.

“Ngojeni kwanza”

“Nini?”

“Kuna nesi alinisaidia naye amekamatwa na hawa watu, nahitaji kuondoka naye”

“Randy kazi yetu ilikuwa ni kuja kukuchukua wewe na tambua kikosi kimetoa zaidi ya dola milioni moja kwa mabadilishano yako, huyu mwanamke achana naye”

Mmoja wa wezangu alizungumza huku akinitazama usoni mwangu kwa macho makali sana.

“Tusiangalie pesa, tuangalie utu, huyu ndio aliye nisaidia hali yangu ilivyo kuwa mbaya. Nahitaji kumsaidia sawa”

“Randy fwata oda ya mkuu sawa”

Nikatazama chumba alicho fungiwa nesi Husna, taratibu nikashusha pumzi nyingi sana.

“Dakika moja”

Nikizungumza huku nikianza kuelekea katika chumba hicho. Wezangu wakasimama huku wakinitazama, nikafika katika chumba hichi, nikawaomba walinzi waweze kunisaidia kufungua mlango ili nizungumze na nesi Husna. Walinzi hawa hakuna ambaye aliweza kunisikiliza, kwani hapa wanalinda kutokana na amri ya mkuu wao na mkuu wao ndio mtu wa pekee ambaye anaweza kuwaamrisha kufungua mlango au kuto kufungua. Kwa bahati nzuri mkuu wao akafika katika eneo hili.

“Samahani mzee ninahitaji kuondoka na huyu nesi, tafadhali ninakuomba unisaidie katika hilo”

“Hahaaa…..RANDY RANDY, unahisi mimi ni kichaa kumuachia mwanamke mzuri kama huyu. Nashukuru sana kwa kuniletea mwanamke mzuri. Wewe ondoka na uniachie huyu mrembo kwa maana nina mpenda sana tena sana”

Maneno ya mzee huyu yakanikasirisha sana, nikatamani kumvamia ila nikajikuta kukishindwa kutokana na vijana wake kuwa na mitutu ya bunduki na wapo makini sana kwa kuimarisha ulinzi wa bosi wao.



“Ondoka usije ukajisababishia matatizo mengine yasiyo kuhusu”

Mzee huyu alizungumza kwa dharau huku akinitazama usoni mwangu.

“Randy, Randy usiniache tafadhali”

Sauti ya nesi Husna ikitokea ndani, machozi ya hasira yakaanza kunilenga lenga.

‘Lazima nirudi kumchukua hata kama ni kwa kuua, ila nitarudi tu’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikianza kutembe kuelekea walipo wezangu.

“Randy”

Mzee huyu aliniita na kunifanya nigeuke na kumtazama.

“Asante sana kwa mtoto mzuri”

Mzee huyu alizungumza huku akiachia kicheko cha kejeli, nikafika katika eneo walilo wezangu, tukaingia ndani ya gari walilo jia na tukaanza safari ya kutoka katika kambi hii.

“Nahitaji kuzungumza na mkuu”

Mwezangu mmoja akatoa simu mfukoni mwake na kunikabidhi. Nikapiga namba ya makao makuu, simu ikaanza kuita baada ya muda ikapokelewa.

“Ndio mkuu, meja Randy ninzungumza”

Ilinibidi nitaje cheo changu cha kijeshi, japo sisi ni kundi la waasi ila tuna vyeo vyetu na sisi.

“Ndio zungumza”

“Mkuu nina kazi ya kumkomboa mwanamke mmoja katika kambi ya hawa walio niteka ninaomba uniruhusu”

“Hivi una akili wewe, tumetoka kukulipia kiasi kikubwa cha pesa, na bado unataka kurudi kwenye kambi hiyo. Hujafanikisha kumleta makamu wa raisi zaidi ya kuwapoteza wezako, bado unatuletea ujinga si ndio?”

Mkuu wangu wa kikosi changu cha mafunzo alizungumza kwa kufoka sana.

“Nalitambua hilo mkuu, ila ninakuomba sana unikabidhi hili, kama ni makamu wa raisi basi nitahakikisha mimimwenyewe namleta mikononi mwenu. Nakuomba sana mkuu”

“Mulienda watano ila ukashindwa, je ukienda mwenyewe utafanyaje eheee?”

“Naomba uni amini mkuu, nahitaji uniidhinishie kwenye hii kazi, nakuahidi sinto kuangusha”

Ukimya ukatawala huku nikisubiria jibu la mkuu wangu wa kazi.

“Mkuu tafadhali niamini”

“Nenda kaifanya, ila ukikamatwa hakika hakuna atakaye kuja kukusaidia wala kutoa kiasi chochote cha pesa kwa ajili yako”

“Asante mkuu”

“Weka loud speaker”

Nikafanya kama alivyo niagiza mkuu.

“Mpeni Randy kila aina ya silaha anayo ihitaji, anakwenda kumkomboa mwanamke anaye mzungumzia. Hakikisheni kwamba muna msubiria hadi pale anapo maliza kazi yake na hakuna kumpa msaada baada ya kushindwa na kazi anayo kwenda kuifanya mumenielewa”

“Sawa mkuu”

“Randy umetoa maisha yako kwa ajili ya mwanamke, ila hakikisha unarudi ukiwa hai sawa”

“Sawa mkuu asante”

Simu ikakatwa na dereva akasimamisha gari.

“Randy unajiamini nini wewe, au ni hisia za kimapenzi ndio zinakurudisha huko?”

“Sio hisia pekee, ila nina hitaji kufanya hili jambo. Yule dada alinisaidia sana mimi kutoka kwenye ile hoteli pasipo kustukiwa kama sio mwana usalama wa Kimarekani, inakuwaje leo hii ninamuacha akiwa mikononi mwa lizee kama lile na limeniahidi kumua?”

“Kwa hiyo kuolewa kwake wewe ndio kuna kuumiza moyo?”

“Si hilo tu, ila nina hitaji kufanya jambo kwa ajili yake”

“Umemsikia mkuu hatuto kupa back up ya aina yoyote, ukifanikiwa au kufeli hilo ni juu yako. Msaada wetu sisi ni silaha, fungua nyuma ya gari huko”

Mmoja wa wezangu alizungumza. Nikashuka kwenye gari, nikazunguka nyuma nikafungua mlango na kukuta silaha kadhaa zikiwa zimepangwa vizuri. Nikachukua bastola nne, mbili nikazichomeka katika miguu yangu eneo la viatu huku moja nikiichomeka nyuma ya kiono changu huku nyingine nikiichomeka katika mifuko ya jaketi kubwa la kuzuia risasi. Nikachukua mabomu kadhaa ya kurusha kwa mkono, kisha nikachukua bunduki aina ya HK416 pamoja na magazine zake zipatazo sita na zilizo jaa risasi. Nikachukua visu viwili, nikaviweka kwenye mifuko ya suruli yangu hii. Nikaongeza magazine sita za bastoka, kisha nikafunga mlango wa gari hili.

“Randy”

 ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

BLOG