Search This Blog

Wednesday, November 18, 2020

POWER SEHEMU YA 9/10

 

 


 POWER

WRITER…………………………………………EDDAZARIA G.MSULWA
WEBSITE………………………………………… www.storyzaeddytz.com
CONTACT……………………………………….. 0657072588/0768516188
AGE……………..18+ 

SEHEMU YA 9 KATI YA 10

 


“Upo getini kwangu!!?”

“Vipi mbona umekuja bila taarifa?”

“Okay ngoja nina kuja”

Romani akakata simu na kunitazama usoni mwangu.

“Inabidi tujifiche usije ukamueleza Qeen kama kuna uwepo wetu humu ndani”

“Sawa mkuu”

“Claudia nenda chumbani. Mimi nina elekea chumba cha Piyanka. Romani hakikisha kwamba Mbilinyi hapigi kelele humo ndani”

“Sawa mkuu”

Tukatawanyika na nikaingia katika chumba alichopo Piyanka. Nikapitiliza hadi dirishani na kufunua pazia, baada ya muda kidogo nikamshuhudia Qeen akishuka kwenye gari na kusalimiana na Romani.

“Kuna nini mbona una chungulia dirishani?”

Piyanka aliniuliza huku akiwa amejawa na wasiwasi kiasi na yeye”

“Kuna mgeni”

“Mgeni, ndio una mkimbia mgeni?”

“Sitaki ujulikane uwepo wetu humu ndani. Nahitaji kila kitu kiwe kimya humu ndani. Umenielewa?”

“Sawa ni nyinyi, mimi kazi yangu inakwenda kimya kimya”

Nikasikia sauti za Romani na Qeen wakizungumza, uzuri ni kwamba chumba hichi kipo karibu na seble hii.

“Umesikia habari ya kutekwa wa yule Mbilinyi aliye kuwa mlinzi wa Ethan?”

“Nimesikia leo kwenye taarifa ya habari”

“Duu yaani sijui ni nani ambaye atakuwa amemteka. Tuachane na hilo, nimekuja na habari ya masikitiko na si nzuri”

“Habari gani hiyo?”

“Latifa amekuwa chizi kabisa. Yaani hapa ninavyo kuambia ni kuimba jina la Ethan, Ethan, Ethan. Hapo ana mdoli wake basi ana muita Ethana weeee. Ana mkumbatia ana lala yane. Ukitaka kugombana naye wewe mpokonye huyo mdoli. Atalia hadi utamuonea huruma.”

Habari hii ikanistua kidogo. Nikatamani kutoka chumbani humu ila nikajizuia ili niweze kusikia ni nini kinacho endele zaidi.

“Heee daktari ana semaje?”

“Dokta amenishauri jambo moja ambalo sijui kama tutafanikiwa kulifanya”

“Jambo gani?”

“Amesema ili Latifa arudi kwenye hali yake ya kawaida ni lazima tuhakikishe kwamba anatafwatwa mwanaume anaye fanana na Ethan vile vile, yaani kuanzia kuzungumza, kutembea na ikiwezekana tumfundishe mambo kadhaa ambayo Ethan alikuwa ana yafanya hapo nyuma ili mradi nafsi ya Latifa irudi kwenye hali yake ya kawaida”

“Mmmm ni mtihani?”

“Kweli Romani. Hapa nilipo nashindwa kufanya kazi, naumia kumuona rafiki yangu akiwa katika hali kama ile. Nihali mbaya sana kwa kweli. Latifa yule aliye kuwa ame nona kipindi kile si Latifa huyu unaye muona hivi sasa, amekondeana. Hali kama zamani, hajitunzi, nywele zipo changu changu.”

Nikamfungua mlango kidogo na kuchungulia, nikamshuhudia Qeen akiwa ameinama chini huku analia kwa uchungu sana. Machozi yakanilenge lenga sana, nikataka kutoka ila nikastukia Piyanka akinishika mkono.

“Muda wa kutoka bado”

Piyanka alizungumza kwa sauti ya chini kiasi.

“Kwa nini?”

“Acha tuimalize hii kazi ndio ujidhihirishe mbele ya hao watu wako. Hivi sasa ni wakati wa wewe kukaa mafichoni acha ibaki siri ya watu wachache”

Nikamtaza Piyanka usoni mwake kwa sekunde kadhaa kisha nikafunga mlango huu na sikuhitaji kuendelea kusikiliza mazungumzo haya ya Romani na Qeen kwani yataendelea kuniumiza moyo wangu. Baada ya kama dakika ishirini hivi, Romani akaingia ndani humu.

“Vipi?”

“Amesha ondoka”

Nikatoka chumbani humu na kumkuta Claudia sebleni.

“Nini tutafanya mkuu juu ya Latifa?”

“Acha tuvumilie”

“Mkuu hembu tazama hii”

Romani akanikabidhi simu yake ambayo ina video inayo muonyesha Latifa hali yake. Hakika nikashindwa kuvumilia na kujikuta nikiondoka sebeleni hapa na kuingia chooni na kujifungia, huku machozi yakinimwagika usoni mwake. Hali aliyo kuwa ana ielezea Qeen ni tofauti kabis ana hai hii ambayo ninayo iona. Hali hii ni tofauti kabisa na niliyo isikia. Latifa ame kuonda sana, ukimtazama lazima uamini kwamba ni mwenda wazimu aliye kosa matunzo japo kuna madaktari wana mtazama kwa ukaribu sana.

‘Nisubirie Latifa, nitakuja kwako mama’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikiendelea kuitazama video hii mara kwa mara hadi nikaizoea. Nikakubaliana na hali halisi pamoja na ushauri wa Piyanka, ni lazima nikae mafichoni hadi nitakapo maliza kazi hii. Nikatoka chooni humu na kumkabidhi Romani simu yake. Nikaelekea jikoni na kuchukua kisu chenye ncha kali na kueleka katika chumba tulicho muweka Mbilinyi.

“Mkuu unataka kufanya nini?”

Romani aliniwahi na kunizuia mlangoni.

“Nahitaji kuzungumza na huyu mpuuzi”

“Na kisu mkononi?”

“Sinto muua sasa hivi. Pisha niingie ndani”

“Ethan, jaribu kuiongoza hasira yako. Kumbuka nini nilikufundisha tukiwa kule porini”

Claudia naye alizunguzma kwa sauti ya upole kidogo, huku naye akiwa amesimama pembeni yangu.

“Nalitambu hilo. Nina waaahidi kwamba simuui huyu mtu ila nahitaji kuzungumza naye”

Romani akanitazama kwa sekunde kadhaa kisha akanipisha mlangoni hapa. Nikaingia ndani ya chumba hichi na kumkuta Mbilinyi akiwa amejawa na mawazo mengi sana.

Sikutaka hata kumuuliza chochote. Nikakishusha kwa nguvu kisu hichi huu ya paja la mguu wa kushoto wa Mbilinyi na kumfanya apige ukunga mkubwa sana huku kisu hichi kikiwa kimeingia nusu nzima.

“Kwausaliti wako, umeyafanya maisha yangu kuwa mabaya mjinga wewe. Umesababisha watu wanao nipenda kuchanganyikiwa na kuwa matahira wakiamini kwamba nimekufa. Eheee”

Nilizungumza huku nikiendelea kukikandamiza kisu hichi kwenye paja la Mbilinyi hadi kikatokea upande wa pili wa paja. Sikujali damu zinazo mtoka, ila nilicho hitaji ni kuituliza akili yangu na machungu yangu kwa kufanya hivi.

“Nilikuamini na kukueleza baadhi ya siri zangu. Nilikufanya kama mkono wangu wa kushoto, ila ilinisaliti tena siku ya furaha katika maisha yangu. Nikiasi gani yule mzee alikuwa ana kulipa eheeee?”

Nilizungumza kwa kufoka. Mbilinyi hakujibu chochote zaidi ya kuendelea kulia kwa maumivu makali sana anayo yapata.

Nikakichomoa kisu hichi na nikajivuta tena ili nichome sehemu nyingine ya paja lake, ila nikastukia mkono wangu ukishikwa kwa nyuma. Nikageuka kwa haraka na kumuona Ethan.

“Acha”

Sura ambayo amekuja nayo Ethan ni sura yangu kabisa, jambo lililo mfanya Mbilinyi kukatisha kilio chake na macho yakamtoka, kwani mimi na Ethan huyu tunafanana kwa kila kitu. Mbilinyi hakumaliza hata dakika moja akazimia kwa hili jambo alilo lishuhudia.

“Kwakufanya hivyo sio kama Latifa ata pona”

“Kwa nini ulimuacha Latifa awe chizi ikiwa wewe ni rafiki yangu. Ehee?”

“Unahisi ningefanya nini? Uliyaka nimtokea katika hali yangu hii ya ujini ili ajue kwamba wewe upo hai?”

Ethan alizungumza huku akinipokonya kisu hichi. Akasimama mbele yangu na kunitazama.

“Akili yako kwa sasa inatakiwa kuangalia ni zoezi gani lililopo mbele yako na si kumtazama huyu Mbilinyi”

“Ethan natambua kwamba una nisaidia. Ila huyu ni adui yangu pia. Laiti kama asinge nisaliti Latifa asinge kuwa kichaa”

“Bora huyo aliye kuwa kichaa. Wapo walio kufa kwa mstuko huko duniani, mara baada ya kusikia kifo chako. Je hao utaweza kuwarudisha duniani kwa kumchoma choma visu huyu?”

Ethan alizungumza kwa msisitizo ulio nifanya mdomo uwe wazi kwani sikuwahi kufikiria kwamba kuna watu duniani wanao nipenda sana hadi kufa kwa mstuko.

“Kazi ya kwenda kutafuta spika zitakazo burudisha katika kampeni, ni lazima uende wewe na usimuagize mtu wa aina yoyote”

“Najua ni wapi zinapo patikana sasa?”

Ethan akanishika mkono wangu wa kulia. Kufumba na kufumbua tukajikuta tupo kwenye gadauni kubwa lililo hifadhia vitu vya kampeni vya chamacha mzee Poul Mkumbo. Tukaziona spika kubwa sana, kabla ya kuzifwata gaduni hili likafunguliwa na wakaingia walinzi kama sita hivi wakiwa wameongozana na mzee Mkumbo pamoja na wapambe wengine wa chama hicho jambo lililo nifanya nitamani kuumaliza uhasama wetu na mzee Poul Mkumbo ndani ya godauni hili.



Nikataka kuwafwata ila Ethan akaniwahi na kunishika mkono wangu.

“Hawajatuona na usifanye chochote”

Ethan alizungumza huku tukiendelea kumtazama mzee Mkumbo pamoja na watu wake jinsi wanavyo endelea kukagua hivi vifaa vya kampeni ikiwemo spika kubwa sana.

“Wapo watu wachache kwa nini tusimvamie hapa hapa ndani tukawaangamiza?”

“Kumbuka gtumeingiaje hivyo sina uwezo wa kufanya hilo unalo lihitaji.”

Mzee Mkumbo na watu wake wakapita pembeni yetu kabisa na hapakuwa na mtu yoyote aliye weza kutuona wala kuhisi uwepo wetu katika eneo hili. Sikuweza kushangazwa na jambo hili kwa maana kwa Ethan ni kitu cha kawaida kutoonekana na watu wengine hata kama nitakuwa naye. Mzee Mkumbo na watu wake walipo maliza kukagua kila kitu wakaondoka eneo hili na kutuacha. Tukatembea hadi upande wenye spika hizi kubwa na Ethan akanionyesha spika ambayo inatakiwa kutegwa bomu kwa ndani. Baada ya kumuhakikishia Ethan kwamba nine weza kuifahamu spika hiyo, tukarudi katika chumba ambacho tulikuwepo na nikamkuta Mbilinyi akiwa bado amepoteza fahamu.

“Pale bomu hili litakapo kamilika hakikisha unakwenda kwenye lile godauni na kijana wako na muna liweka hilo bomu”

“Sasa mimi nina fahamu hilo gadauni ni sehemu gani lilipo

“Nitawaonyesha ni sehemu gani godauni hilo lina patikana.”

Ethan hakuhitaji nimuulize swali jengine. Akapotea na kuniacha nikiwa katika wakati mgumu wa kufikiria ni kitu gani ambacho nitaweza kukifanya katika mpango wa kuhakikisha kwamba, kabla sijamuua mzee Mkumbo ni lazima nihakikishe ana fahamu kwamba mimi ndio ninaye mua.

“Mkuu”

Romani aliniita huku akiingia ndani humu.

“Ndio”

“Tunaweza kuzungumza?”

Romani alizungumza kwa upple huku akimtazama Mbilinyi ambaye bado mguu wake unandelea kumwagikwa na damu nyingi.

“Tuzungumze”

“Yule binti ameniomba ombi moja “

“Ombi gani?”

“Anahitaji kumfanyia majaribio huyu jama juu ya bomu hilo. Je inawezekana”

Nikamtazama Mbilinyi ambaye bado amepoteza fahamu zake. Nikatoka ndani humu pasipo kumjibu Romani jambo lolote. Nikakutana na Piyanka akitoka katika chumba anacho fanyia kazi.

“Nasikia unahitaji kumfanyia majaribio Mbilinyi?”

“Yaa nahitaji kumjaribu yeye kwani ana faida yoyote kwako?”

Nikapata kigugumizi kizito sana, japo ni kweli Mbilinyi amenisaliti, ila kuna baadhi ya mambo mema katika enzi za urafiki wetu aliweza kunishauri kwa upole sana.

“Mbona kimya”

“Nahitaji kulifikiria hili kwa umakini sana hilo jambo”

“Sawa”

“Unakwenda wapi?”

“Na mimi ninakwenda kupata kifungua kinywa”

Piyanka akanipita na kuelekea kupata kifungua kinywa. Nikaingia chumbani kwetu na kumkuta Claudia akiwa amekaa kitandani huku akiwa katika hali ya upole sana.

“Vipi mbona upo katika hali ya unyonge?”

“Nina omba niweze kukuuliza swali Ethan”

“Sawa unaweza kuniuliza tu”

“Hivi kweli nina haki ya kuwa na wewe kimahusiano?”

Swali la Claudia likanistua kidogo na nikamtazama usoni mwake kwa umakini sana.

“Una maanisha nini?”

“Nina maanisha kwamba. Yupo mwanamke ambaye ana kupenda. Yupo mwanamke ambaye amechanganyikiwa kwa ajili yako. Wewe ndio wa pekee ambaye unaweza kumrudisha yeye katika hali yake ya kawaida. Tafadhali Ethan nina kuomba sana, niweze kumuachia nafasi msichana huyo”

Hakika nikajikuta nikiwa mnyonge, nikakosa jambo la kuzungumza kwa Claudia mwanamke ambaye alikuwa ana ishi maisha kama mnyama na hakuwa ana elewa ni nini kinacho endelea huku duniani. Ila kwa muda mfupi tu amekuwa na uwezo mkubwa sana wa akili na anajua nini anacho kifanya.

“Kwa nini umeamua kuzungumza maneno kama hayo?”

“Ethan ngoja nikuambie ukweli wa moyo wangu”

Claudia akakaa kimya kwa sekunde kadhaa huku akinitazama usoni mwangu.

“Moyo wangu umetokea kumpenda sana Romani kuliko wewe. Natambua wewe ni mwanaume wangu wa kwanza ila sijakupenda kama ninavyo mpenda sana Romani. Natambua haya maneno ni magumu sana kwako ila ina kuomba usinielewe vibaya katika hilo. Wala usimfikirie Romani vibaya kwa maana hajawahi kuniambie chochote kinacho husiana na mahusiano ila ananiheshimu kama shemeji yake”

Nikahisi mwili mzima ukipoteza nguvu. Nikamtazama Claudia usoni mwake na kushindwa hata nimjibu kitu gani, nikashindwa kuzungumza chochote.

“Ethan nisamehe sana kwa hayo. Ila nilicho kuambia ni jambo la ukweli kabisa kutoka moyoni mwangu”

“Nimekuelewa”

Nilizungumzwa kwa upole kisha nikatoka chumbani hapa. Nikatoka kabisa nje na kukaa kwenye moja ya bustani iliyopo katika nyumba hii. Nikaanza kukumbuka kumbukumbu za maisha ya nyuma niliyo pitia na Claudia. Japo ni maamuzi magumu aliyo yafanya ila sina namna zaidi ya kukubaliana na ombi lake kwa maana yupo Latifa pamoja na Hawa wote wana nisubiria mimi.

Nikiwa katika eneo hili la bustani nikamuona Romani akija huku mikononi mwake akiwa ameshika chupa pamoja na glasi mbili. Akakaa katika kiti cha pembeni yangu na kuiweka chupa hii ya pombe kali karibu yangu.

“Natambua unapitia kipindi kigumu mkuu. Ila tushiriki kinywaji pamoja kama huto jali”

Nikamtazama kwa sekunde kadhaa Romani kisha nikamkubalia kwa kumtingishia kichwa. Romani akamimina kiasi kidogo cha pombe hii kali kwa kila glasi kisha akanikabidhi glasi yangu.

“Chease”

Romani alizungumza huku tukigonganisha glasi zetu kwa pamoja. Kisha tukapiga funda moja ambalo hakikia nilipo imeza nikahisi kama koo langu lina chanwa chanwa kwa viwembe.

“Khaaa fuc**”

Nilizungumza huku nikitingisha kichwa.

“Hii pombe ni kali sana. Huwa nina kunywa nusu glasi tu kukiweka kichwa sawa”

Romani alizungumza huku akinitazama kwa macho yaliyo jaa uwekundu.

“Romani”

“Ndio mkuu”

“Una demu”

“Mmmm hapana”

“Mbona mmmm kisha hapana?”

“Bado sijakuwa kwenye mahusiano ya kueleweka.”

“Unaweza kuwa kwenye mahusiano ya kuweleka lini?”

“Bado sijajua mkuu, si unatambua wanawake wenyewe wanapenda pesa kuliko maisha ya mwanaume”

“Sasa kuna mwanamke ana kupenda”

“Mwanamke anaye nipenda mimi. Atatokea wapi mkuu ikiwa mimia majiona ni mtu ambaye sina bahati kabisa kwneye maisha yangu”

“Una bahati”

“Mmmm!!”

“Ila mtu huyo sinto hitaji umuumize moyo wake.”

Romani akakaa kimya huku akinitazama usoni. Nikapiga fumba jengine ambalo likapelekea kumaliza wisky hii.

“Ni nani huyo?”

“Claudia ana kupenda sana. Ana kuhitaji uwe mpenzi wake”

Romani macho yakamtoka kwa maana siku zote amemuheshimu sana Claudia.

“Mkuu ume lewa haraka hii?”

“Hapana ninacho kizungumza ni kitu ambacho kina toka moyoni mwangu. Claudia ana kupenda kuliko anavyo nipenda mimi. Nahisi unatambua jinsi Claudi anavyo pata shinda kwa ajili yangu hivyo hakikisha kwamba una utunza moyo wa Claudia vizuri”

“Mkuu unajua nina kuheshimu sana. Hujawahi kunitania kwenye maisha yako yote. Hembu niambie katika hili, akili yako niyo ni pombe au ni akili yako ya kawaida?”

“NI akili yangu ya kawaida kabisa. Hakikisha kwamba una mpenda Claudia na usiku wa leo nahitaji ukalale kwake”

“Mkuu”

“Sio ombi ni amri. Hakikisha kwamba humuumizi Claudia.”

Baada ya kumaliza kuzungumza maneno hayo nikanyanyuka na kuondoka eneo hili. Nikakutana na Claudia sebleni akiwa mpole sana.

“Romani leo atakuwa ni mgeni wako chumbani kwetu”

Nilimuambia Claudia kwa upole kabisa kisha nikaelekea katika chumba cha Mbilinyi. Nikavuta kiti na kukaa pembeni ya kitanda hichi huku nikiendelea kumtazama jinsi alivyo lala. Nikakitazama kikombe cha chai kilichopo pembeni yangu, nikakiokota kisha nikamwagia chai hii ya baridi usoni mwa. Mbilinyi akaanza kupepesa pepesa macho yake kisha akayafumbua.

“Amka”

Nilimuambia Mbilinyi huku nikimpiga piga makofi shavuni mwake.

“Una nafasi ya mwisho kwenye maisha yako”

“Ethan”

“Ndio una jambo unaho hitaji kuniambia?”

“Hata nikifa leo. Ila huto weza kumuua mzee Mkumbo”

“Hivi kumbe wewe ni mgumu kiasi hichi ehee. Sawa mimi sihitaji maneno mengi sana kwako ila sinto kuua hadi uweze kushuhudia jinsi mkuu wako anavyo kufa”

Baada ya kuzungumza maneno hayo nikanyanyuka na kutoka ndani humu. Nikiwa nina elekea chumbani kwa Piyanka nikajikuta nikisimama katika mlango wa chumba nilicho kuwa nina lala na Claudia. Nikaanza kusikia miguno ya kimahaba ambayo hakika ikaifanya roho yangu kuniuma kisawa sawa. Kwani miguno hii ni ya Romani na Claudia. Hasira ikanipanda, nikatamani kufungua mlango wa chumba hichi ila nikajikuta nikijizuia. Nikapiga hatua na kuingia katika chumba cha Piyanka bila ya kugonga mlango.

“Umenistua sana Ethan”

“Kwani kuna ubaya wa mimi kuingia hapa bila ya kubisha hodi?”

“Tuachane na hilo. Kwasasa bomu lipo hatua za mwisho umefikia wapi kwa ajili ya kumfanyia mtu majaribio?”

Nikamsogelea Piyanka kwa nyuma na kumkumbatia kwa nguvu huku nikitoa mihemo ya asira sana.

“Ethan una fanya nini?”

Nikamjibu Piyanka kwa vitendo kwani kitu nilicho mfanyia ni kufungua kifungo cha suruali yake kisha nikaishusha chini na kuanza kuyatomasa tomasa makalio yake.



“Ethan Ethan tafadhali nipo katika muda wa kufikiria. Nakuomba uniache”

Piyanka alizungumza huku akipandisha suruali yake. Akajitoa mwilini mwangu na kusimama futi kadhaa kutoka sehemu nilipo kaa mimi.

“Umekunywa eheee?”

“Hapana”

“Hapana wapi Ethan ikiwa nina kusikia kabisa una nukia harufu za pombe kinywani mwako. Nakuomba utoke basi nikimbizane na muda niweze kumaliza bomu hili. Kumbuka kwamba kesho kutwa Mkumbo ana mkutano Jangwani”

Nikamtazama Piyanka kwa sekunde kadhaa kisha nikatoka ndani humu. Hakika siku ya leo sikuwa na furaha ya aina yoyote. Nikarudi sebleni na kukuta chupa ya pombe ambayo tulikuwa tuna itumia mimi na Romani. Sikujali kama ina ukali wa kiasi gani moyoni mwangu. Nilicho kifanya ni kuanza kuinywa kwa fujo hadi nikaanza kuhisi kama dunia ina mzunguko wa tofauti. Hali ya kuto jielewa ikanitawala sana kichwani mwangu na mwishowe, nikahisi giza zito sana likitawala katika macho yangu na mwishowe nika lala usingizi fofofo.

***

Taratibu nikayafumbua macho yangu na mtu wa kwanza kumuona ni Romani aliye simama pembeni yangu.

“Unajisikiaje mkuu?”

Taratibu nikaka kitako huku nikimtazama Romani usoni mwake. Akanikabidhi mfuko wa lailoni ambao ndani umefungwa barafu. Kutokana na maumivu makali ya kichwa, nikajibandika mfuko huu kwenye paji langu la uso na maumivu kidogo yakapungua.

“Kuna supu hapa nimekuandalia mkuu. Najua hapo utakuwa una hang over kubwa.”

“Leo ni lini?”

“Leo ni ijumaa kesho ndio siku ambayo mkutano wa mzee Mkumbo una fanyika”

“Saa ngapi sasa hivi?”

“Ni saa nane mchana”

“Saa nane mchana!!!”

Nikasimama huku nikihisi kuchanganyikiwa kwani kama kesho ni mkutano mkubwa wa kampeni za mzee Mkumbo basi nina uhakika maandalizi ya kuzipeleka spika zile katika kiwanja cha kampeni tayari zimesha fanyika.

“Piyanka yupo wapi?”

“Ndani”

Nikaelekea chumba cha Piyanka na kumkuta akiwa anafunga nati ndogo katika bomu alilo litengeneza.

“Umemaliza?”

“Ndio ninamalizia kufunga nati ya mwisho”

“Ehee nieleze matumizi ya bomu hili”

“Kuna simu hii unaweza kuitumia kuhakikisha kwamba una lipua bomu hilo”

Biyanka alizungumza huku akinikabidhi simu ndogo ya kawaida sana.

“Ukiminya kitufe cha kupiga. Bomu linaanza kufanya kazi, ukiminya kitufe cha kukatia simu bomu linasimama. Na bomu hili nimelitega kwa sekunde thelethini hadi kulipuka”

“Ahaa sawa”

“Ulipukaji wake ni wa tofauti sana. Halitoi mlipuko kama mabomu mengine. Ila bomu hili likilipuka linatoa gesi ambayo ndio itakayo samba kwenye hewa na kuwaua watu”

“Na mtu anakufa kwa muda gani mara baada ya kuvuta gesi hiyo?”

“Ndani ya sekunde stini tu. Kama atakuwa hajapata matibabu ya haraka sana basi anaangamia”

“Matibabu ya haraka hapo ni yapi?”

“Kuna hii dawa, nimeitengeneza. Kama utahitaji wewe kwenda uwanjani hapo ni lazima uhakikishe kwamba una jichoma sindano ya dawa hii. Hata utakapo vuta hewa nyenye gesi ya sumu basi huto weza kuudhurika”

“Hii hewa itasamaa kwa upana gani?”

“Mmmmm nimagadiria upana wa viwanja vitatu vya mpirwa wa miguu. Hivyo ni kamam mita mia tatu. Hivyo viumbe vyote vilivyomo ndani ya mita mia tatu. Vitakufa”

“Ni upana na urefu au upana tu wa mita mia tatu?”

“Yaani upana na urefu vyote ni mita mia tatu”

“Hapo sawa. Ila kama nilivyo kuambia nina hitaji kuhakikisha nina mteka mzee Mkumbo”

“Sawa unaweza kupata nafasi hiyo”

“Kitu kingine unaweza kutengeneza bomu la ziada ambalo linaweza kumuua mzee mkumbo peke yake?”

“Hapana ila kuna vichupa hivi vitano ambavyo vina gesi hii ya sumu. Endapo utakifungua watu walio karibu na eneo hilo basi wata kufa”

“Sawa”

Baada ya Piyanka kunieleza matumizi yote ya hili bomu. Akanikabidhi rasmi na nikawaita Claudia na Romani na wao wakapatiwa somo hili na Piyanka. Tukachoma sindano ambazo zitatukinga katika kuathirika na mlipuko wa bomu hili.

“Mkuu mimi nina mpango ambao nina imani kwamba utakuwa ni mzuri”

“Nieleze”

“Nilifikiria tutafute gari moja la wagonjwa. Mimi na Claudia tutaelekea pale uwanjani kama wauguzi, nina imani hatuto tiliwa mashaka. Bomu mara baada ya kulipuka na watu kuanguka anguka, tutakaye muwahi sisi ni mzee Mkumbo. Tutamkamata na tutamchoma sindano hii ili asiweze kuudhurika”

“Piyanka sasa kama mzee huyo atachomwa sindao itakuwaje kwa mara ya pili kama nikihitaji kumuu kwa hii sumu?”

“Hilo sikuweza kulifikiria kwa haraka. Inabidi umuue kwa silaha tu”

Tukabaki kimya huku kila mtu akimtazama mwenzake usoni.

“Sawa. Romani mutanihakikishia kwamba muna mutamleta mzee Mkumbo mikononi mwangu”

“Ndio mkuu nitahakikisha kwamba ana kuja mikononi mwako”

“Sawa, mimi leo nitahakikisha kwamba nina kwenda kuliingiza bomu hili ndani ya spika ambayo itakuwa miongoni mwa spika zitakazo kuwa uwanjani”

“Sawa sawa mkuu”

Baada ya maumivu ya kichwa changu kuniisha, nikajiandaa huku nikiwa nimevalia nguo nyeusi tupu pamoja na kofia nyeusi ambayo kwa haraka haraka siwezi kufahamika kwa watu. Nikaliingiza bomu hili katika begi dogo la mgongoni.

“Upo tayari”

Niliisikia sauti ya Ethan ikinisemesha, nyuma yangu. Nikageuka na kumkuta akiwa amesimama mlangoni mwa chumba changu.

“Ndio”

“HIi ni ramani ya lile godauni lilipo”

“Unataka kuniambia kwamba hadi sasa hivi zile spika hazijapelekwa uwanjani?”

“Ndio. Spika zitapelekwa usiku wa leo katika kiwanja hicho”

“Utakuwa pamoja nami?”

“Hapana hii kazi ni yako wewe unatakiwa kuwa makini. Nenda usiku wa saa mbili, hakikisha unakuwa makini. Kitambaa hichi hakikisha una funika uso wake. Na hivi ni vifaa ambavyo vitakusaidia kuingia ndani ya godauni lile”

Ethan akanikabidhi mfuko wa plastiki ambao nilipo utazama kwa ndani nikaona bisibisi pamoja na tochi. Nikakichukua na kitambaa hichi kikubwa kiasi na kujaribu kukifunga usoni mwangu.

“Kinapendeza”

“Yaaa kimekupendeza huto julikana. Nakutakia kazi njema na umakini”

Ethan akapotea mbele yanguna kuniacha peke yangu ndani humu. Kutokana yamasalia masaa mawili kabla ya kufika usiku wa saa mbili ikanilazimu kukaa ndani humu hadi majira ya saa mbili usiku. Nikawaaga Romani, Piyank a na Claudia. Ila kabla ya kuondoka nikaingia katika chumba tulicho mfungia Mbilimyi.

“Nina imani kwamba kesho utaweza kumshuhudia bosi wako unaye muamini na kumtukuza akiingia na utashuhudia kifo chake”

“Hahaa unahisi kwamba utaweza kufanikisha hilo”

“Subiri uone. Kitu kingine ambacho kitakufanya uweze kuzungumza vizuri ni mke wako na mwanao”

Mbilinyi akastuka sana japo kuwa sifahamu ni wapi ilipo familia yake ila kwa kuzungumza hivyo kumemfanya apoteze ujasiri mbele ya uso wangu.

“Ethan?”

“Hakuna cha Ethan. Nitahakikisha kwamba ninakufuta wewe na kizazi chako. Mkumbo na kizazi chake”

Nikatoka ndani humu na kuelekea nje na kumkuta Romani akiwa ananisubiria pembeni ya gari lake jengine aina ya Toyota Alteza.

“Mkuu kuwa makini”

“Sawa hakikisha kwamba huyo mwana haramu munampatia chakula”

“Nitafanya hivyo”

Nikaingia kwenye gari na kuondoka eneo hili na kuianza kuifwata ramani aliyo nipatia Ethan. Ramani hii ikanitoa nje kabisa ya jiji la Dar es Salaama. Nikafika katika eneo katikati ya Bagamoyo na Dar es Salaam. Nikakunja kulia kwangu na kuifwata barabara ya vumbi hadi karibu kabisa na eneo lilipo godauni hilo. Nikaificha gari porini, kwani eneola godauni hilo kuna ulinzi mkali sana. Nilashuka kwenye gari na kujifunga kitambaa hichi husoni mwangu, nikatembea katika msitu huu ulipo pembezoni mwa hili godauni na kufika eneo lilipo godauni. Nikapanda katika mti mmoja mrefu ulipo pembezoni mwa godauni. Nikafika juu kabisa ya mti huu na nikafanikiwa kupanda juu ya jengo hili la godauni pasipo mlinzi wa aina yoyote kuweza kunistukia. Kutokana ramani ya jengi hili nimeihifadhi kichwani muda mchache kabla ya kufika hapa. Nikafika katika sehemu ambayo hata nikilikata bati lake sio rahisi kwa walinzi kunisikia. Nikavua begi langu la mgongoni na kutoa mkasi maalumu wa kukatia bati. Nikalikata kwa umakinia na usawa ambao ninaweza kuingia mimi.

Nikaingia ndani ya godauni hili na kukuta idadi ya vitu vikiwa vimepungua sana tofauti na pale awali nilivyo pakuta. Nikaelekea katika eneo ambalo lina spika nne kubwa. Kwaharaka nikatoa bisibisi ndefu na kubwa kiasi, nikaanza kuifungua spika hii, sikuchukua muda mrefu sana nikafanikiwa kuifungua yote.

Nikalitega bomu hili sehemu ambayo hata ukichungulia kwa kupitia eneo la mbele la hii spika huto weza liona bomu hili. Nikaliwasha kisha nikaifunga spika hii kama nilivyo ikuta.

Nikiwa katika harakati za kutoka ndani humu, nikastukia mlango mkubwa wa godauni hili ukifunguliwa jambo lililo nifanya niwahi kujibanza kwenye viti vingi vilivyomo humu ndani. Nikaizima tochi yangu na taa zote humu ndani zikawashwa. Nikasikia mngurumo wa gari, kwa upanyo wa viti hivi nikashuhudia gari aina ya scania likiingia ndani humu huku likiwa lina kontena kubwa. Gari hilo likasimama mita chache kutoka sehemu zilipo sipika hizi na wakashuka vijana nane walio jazia misuli yao na taratibu wakaanza kubeba spika moja baada ya nyingine.

Vijana hawa wahakuweza kupata hisia yoyote ya uwepo wangu humu ndani. Walipo maliza kuziingiza spika zote nnne wakaingia kwenye kontena hili huku nami kwa haraka nikikimbilia gari lao na kujivirigisha chini ya uvungu wa hili lori na kushikilia vyuma vilivyopo chini ya hili lori. Taratibu lori hili likatoka katika eneo hili na kuianza safari ya kuelekea mjini kwa mwendo wa taratibu. Nilipo fika katika eneo ambalo nililiacha gari nikaachia vyuma hivi na kutua chini. Lori lilipo pita nikachuchumaa na kutazama eneo hili kwa umakini na sikuweza kupotea. Nikakimbilia msituni na kulikuta gari langu likiwa katika hali ya usalama.

Nikaingia ndani ya gari, nikaa kwa takribani dakika ishirini ili kuipa nafasi lori hili kufika barabara kuu. NIlipo hisi kwamba muda huu umetosha, nikawasha gari na kuondoka na kuianza safari ya kurudi jijini Dar es Salaam. Nikiwa njiani nikalipita lori hili na nikajikuta nikitabasamu mimi mwenyewe kwani hii kazi niliyo inazisha inakwenda kukamilika.

Wazo la familia ya Mbilinyi likanijia akilini mwangu. Nikajaribu kutafakari ni wapi wanaweza kuwa, jibu liatua ni katika nyumba ambayo nilikuwa nina ishi mimi na Biyanka.

“Ethan”

Niliita na baada ya sekunde kadhaa nikamshuhudia Ethan akiwa amekaa siti ya nyuma.

“Vipi?”

“Niwapi ninaweza kumpata mke wa Mbilinyi”

“Sehemu uliyo ifikiria ndipo walipo?”

“Nitaingiaje ndani mule ikiwa ulinzi wa ile nyumba si wa kitoto?”

“Ni kweli ila kazi hiyo unayo taka kuifanya ni hatari. Ila acha nikakusaidie”

“Kweli?”

Ethan wala hakusubiria kunijibu akapotea ndani ya gari langu. Nilipo mataa ya mwenge nikastukia kumuona Ethan akiwa amekaa siti ya mbele, akanipa ishara nitazame nyuma. Nikamshuhudia mke wa Mbilinyi pamoja na mwanaye wakiwa wamelala.

“Umewapataje?”

“Unaniuliza nimewapataje ikiwa nina uwezo wa kukuzidi wewe binadamu?”

“Sawa bwana nimuekuelewa”

Nilizungumza huku nikiwa nimejawa na tabasamu pana usoni mwangu. Tukafika nyumbani pamoja na Romani akanifungulia geti na kuingia ndani.

“Hakikisha kwamba huwai hawa. Hawana makosa yoyote”

“Ila huyu mume wake ni msaliti”

“Nalitambua hilo na japo pia alikiwa anafahamu mpango wa kutekwa kwako kipindi kile ila alihitaji kukusaidia, ila akashindwa kwa maana yeye ni mwanamke na ameolewa ndio maana waliondoka ukumbini mapema sana kuliko watu wengine nahuku nyuma ndio wakaachia dhahama hiyo.”

“Nimekuelewa”

Ethan akatoweka ndani ya gari. Nikashuka na kufungua mlango wa nyuma. Romani akachungulia na kustuka kidogo.

“Huyu si mke wa Mbilinyi?”

“Ndio ni mke wake”

“Umemtolea wapi?”

“Nitakuambia. Waingize ndani kwa Mbilinyi wote wawili”

Nikaelekea ndani, nikamkuta Piyanka sebleni akiwa ameshika kikombe chenye kahawa.

“Hulali?”

“Siwezi kulala hadi kazi iishe kabisa”

Piyanka akashangaa kumuona mwamke akiingizwa katika moja ya chumba huku akiwa amepoteza fahamu zake.

“Yule ni nani?”

“Mke wa aliye kuwa mlinzi wangu mmoja hivi”

“Ahaa….imekuwaje ameletwa humu akiwa katika hali ile?”

“Nahisi unatambua nilisalitiwa?”

“Ndio”

“Na mlinzi wangu wa karibu?”

“Ndio”

“Basi yule ndio mke wake”

“Ahaa, sasa unalipiza kisasi kwa mke wake?”

“Piyanka utajua kila jambo litakapo fika tamati.”

Nikaingia katika chumba cha Mbilinyi na kumkuta akimuita mke wake, ila mke wake wala mwanaye hapakuwa na aliye weza kuitikia.

“Umewafanya nini wapendwa wangu?”

Mbilinyi aliniuliza kwa jazba kubwa huku akinikazia macho. Ubaya ni kwamba hawezi kufanya chochote kutokana mikono na miguu yake imefungwa na pingu.

“Nahitaji uweze kupata maumivu kama yake maumivu niliyo yapata mimi kwenye maisha yangu”

Nilizungumza kwa sauti ya upole na nikatoa sindano moja ambayo ina dawa ya kuzuia kuathirika na sumu ya bomu la nyukli tulilo litega katika moja ya spika. Nikamtazama Mbilinyi jinsi macho yanavyo mtoka kwa woga, kisha nikashika mwanaye na kumtazama vizuri shingoni mwake kisha nikamchoma sindano hii kwa nguvu shingoni mwake na kuisukuma dawa yote jambo lililo mfanya Mbilinyi kuliwa kwa uchungu sana akiamini kwamba sindano hiyo niliyo mchoma mwanaye ni sumu ambayo inaweza kumpotezea uhai wake.



“Baada ya muda mchache mapigo ya moyo ya mwanao yanakwenda kusimama na kutulia tuli. Namuonea huruma kwa maana ana kufa akiwa bado mdogo sana na yote hayo baba ndio ana yasababisha. Naamini wewe kwa mikono yako ndio umesababisha mimi kufikia hapa”

Nilizungumzwa kwa suati ya upole huku nikimtazama Mbilinyi jinsi anavyo hangaika hangaika kujitoa kwenye pingu hizi ila anashindwa kufanya hivyo.

“Utaendelea kuhuhudia familia yako ikiteketea taratibu. Sikupenda hata siku moja niweze kumuangamiza huyu malaika ambaye hajui ni nini kinacho endelea hapa duniani. Ila sina jinsi zaidi ya kufuta maadui zangu pamoja na familia zao”

Mbilinyi akaendelea kugugumia kwa maumivu ya kulia. Nikamuita Romani na nikamuomba aweze kumtoa mtoto wa Mbilinyi humu ndani na Romani akatekeleza.

“Mke wako ni mzuri sana. Ni kabila gani la kitanzania?”

Nilizungumza huku nikizishika shika nywele za mke wake.

“Don’t touch my wife?”

“Mmmm nisimguse mke wako, kwa nini?”

“Hajakukosea yeye. Wewe pambana na mimi na sio yeye?”

“Nipambane na wewe hahaaa. Nitaangalia nini cha kumfanya”

Nikajitahidi na kumbeba mke wa Mbilinyi na kutoka naye ndani humu. Nikamkuta Romani akiwa na mtoto wa Mbilinyi, sebleni akisubiria amri yangu”

“Kuna vyumba ambavyo havitumiki?”

“Ndio mkuu”

“Tuwafungie hawa na hakikisha kwamba hawaonekani na Mbilinyi”

“Sawa”

Romani akaongoza hadi kwenye chumba ambacho hakitumiki. Tukawalaza mke wa Mbilinyi pamoa na mwanaye kitandani, kisha tukatoka ndani humu.

“Mkuu nimefanikiwa kupata ile gari ya wagonjwa pamoja na mavazi?”

“Ni gari ya hospitali gani hapa Dar?”

“Muhimbili”

“Vitambulisho?”

“Pia tumefanikiwa kuvipata”

Tulizungumza na Romani huku tukiwa tumesimama kwenye kordo hii.

“Nakuamini Romani hakikisha hii kazi inakwenda vizuri”

“Usijali mkuu nitahakikisha kwamba una furahi”

“Nashukuru”

“Mkuu”

“Ndio”

“Ninashukuru”

“Kwa nini unanishukuru?”

“Katika wanaume watofauti sana hapa duniani. Wewe ni mmoja wa wapo. Kwenye maisha yangu sikutarajia kama unaweza kufanya ulicho nifanyia kwa Claudia”

Nikamtazama Romani usoni mwake huku moyoni mwangu nikijikaza kuutoa wivu wangu wa kupokonywa mwanamke na mfanyakazi wangu.

“Usijali kwenye maisha hayo mambo yapo. Sikutaka kuudhulumu moyo wa Claudia na wala sikuhitaji kuzuia hisia zake kwako. Ni vyema alivyo niambia mapema na nikafanya maamuzi kuliko jinsi ambavyo angejaribu kuchepuka na kujikuta akitugombanisha”

“Ni kweli mkuu. Ni maamuzi magumu ila nina shukuru”

“Sawa, nenda kapumzike, ili ujiweke sawa na kazi ya kesho”

“Poa”

Nikaingia chumbani kwangu, nikabadilisha nguo hizi nilizo toka nazo kufanya kazi kisha nikaoga na kuvaa nguo za kulalia. Sauti ya mlango wangu kugongwa kwa utaratibu ukanifanya niutazame kwa sekunde kadhaa kisha nikausogelea na kuufungua na kukutana na sura ya Piyanka ambaye naye amevalia nguo za kulala.

“Mmmm ninaweza kuingia?”

“Ndio”

Nikaufungua mlango na Piyanka akaingia ndani humu na kuanza kukitazama tazama chumba hichi.

“Niambie hivi ulifanikiwa kufanyiwa ule upasuaji?”

“Yaa Mungu alisaidia, ulifanikiwa kwa kiasi kikubwa na sasa hivi nipo sawa kama wanawake wengine.”

“Hongera sana”

“Ninaweza kuleta wyne tukanywa pamoja?”

“Mmmm sawa”

Piyanka akatoka ndani humu, huku nikiwa tayari nimesha litambua lengo la yeye kuja chumbani kwangu. Baada ya dakika kadhaa akarudi akiwa ameshika chupa ya wyne pamoja na glasi mbili. Tukakaa kwenye sofa mbili za mtu mmoja mmoja zilizomo ndani ya chumba hichi. Akamimina kiasi cha kutosha kwenye kila glasi kisha akanipatia glasi yangu.

“Ethan”

“Naam”

“Imekuwaje ukamkabidhi Romani mwanamke wako?”

“Sijamkabidhi, ila Claudia ana upendo mkbwa kwa Romani kuliko mimi. Hivyo nimeona sio vizuri kuzuia hisia za mtu ambaye tayari alisha kudhihirishia kwamba ana mtu ana mpenda”

“Ahaa sawa. Je moyoni mwako ina kuumiza?”

“Kwa kiasi fulani ila nimeridhika kwa hilo.”

Tukaendelea kuzungumza mambo mengi sana ambayo yanahusiana na biashara zetu. Pia tukapenda kushirikiana kwenye biashara nyingi mara tu matatizo haya yatakapo pungua au kwisha kabisa. Wyne hii taratibu ikazidi kuzididha kilevi kwenye kichwa changu na kujikuta nikimshika Piyanka mkono wake wa kulia na kumvutia karibu yangu.

“Ethan bwana”

Piyanka alilalama mara baada ya kumtomasa maziwa yake. Nikafungua kifungo cha shati lake ambalo ni jepesi kiasi kisha nikaanza kuyanyonya maziwa yake ambayo hatakufunikwa hata na sidiria. Vilio vya kimahaba vya Piyanka vikachochoea kuongeza manjonjo yangu katika kuhakikisha kwamba ninampa burudani ambayo hakika hato ijutia kuipata. Ndani ya muda mchache tukajikuta tukiwa katika raha ambayo sikuzote haielezeki. Tukaburudishana hadi kila mtu akaridhika na nafsi yake, kutokana na uchovu wa pombe pamoja na mtanange wote tukajikuta tukipitiwa na usingizi na kulala fofo.

***

Siku iliyo fwata, mimi na timu yangu ya watu watatu ambao ni Claudia, Piyanka na Romani, tumejipanga kisawa sawa kuhakikisha kwamba leo inakwenda kuwa siku kubwa ya vilio kwa mamia ya watu watakao hudhuria katika viwanja vya jangwani ili kumsikiliza mzee Poul Mkumbo. Nikaingia katika chumba cha mke wa Mbilinyi na kuwakuta wakiwa wamekaa kitandani yeye na mwanaye. Wote walipo niona walishustuka sana, mke wa Mbilinyi akatamani kuniita ila mdomo ukajawa na kigugumizi.

“Ba mdogo Ethan”

Mtoto wa Mbilinyi alizungumza huku akiwa amejawa na tabasamu pana sana. Akashuka kitandani, akanikimbilia na kunikumbatia kwa nguvu. Taratibu nikachuchuma na kumtazama usoni mwake, huku nami nikiwa na tabasamu feki.

“Ethan?”

“Niambie shemeji?”

Nilizungumza kwa sauti ya upole sana ili mtoto wa Mbilinyi asiweze kuelewa ni jambo gani ambalo linaendelea.

“Ni macho yangu au nipo usingizini bado kwa maana nilipo lala ni tofauti na nilipo amka au nimefariki na hapa ni peponi?”

Mke wa Mbilinyi aliniauliza maswali mengi ya mfululizo huku mwengine yakiwa yananifurahisha.

“Kwa nini ufariki ikiwa muda wa wewe kufariki haujafika?”

“Si niliambiwa kwamba umefariki dunia Shemeji?”

“Hapana nipo hai kama ulivyo niaona. Nilivyo sikia habari ya kutekwa kwa rafiki yangu kidogo ilinistua na nikaona kwamba halitokuwa jambo zuri kama sinto fanya jambo ambalo litahakikisha nyinyi munakuwa salama”

“Ohoo asante shemeji. Vipi hujafahamu ni wapi alipo mume wangu?”

“Hapana ila vijana wangu wana endelea kuifanya kazi yao kuhakikisha kwamba wana jitahidi kumpata akiwa hai au amekufa”

“Nashukuru sana shemeji. Mungu azidi kukubariki kwa kila jambo ambalo una lifanya”

Mke wa Mbilinyi alijikuta akinibariki pasipo kufahamu kwamba mimi ndio mtu wa pekee ambaye nimemteka mume wake.

“Amen. Acha niwaandalie kitu cha kuweza kula kidogo”

“Sawa shemeji una onaje nikakusaidia?”

“Hapana shemeji sio vyema mukatoka ndani humu kwa maana watu wabaya bado wana endelea kuwasaka. Hivyo sinto hitaji muingie matatizoni. Hivi siku ambayo alivamiwa Mbilinyi nyumbani kwake. Wewe na mtoto mulikuwa wapi?”

“Tulikuwa Mbagala kwa mama. Tena siku hiyo tuliondoka mchana kabla ya tukio kutokea.”

Mke wa Mbilinyi alizungumza kwa upole ulio changanyikana na majonzi mengi.

“Pole sana shemeji”

“Asante. Ila shemeji naomba niweze kukuomba msamaha wa jambo ambalo siku zote liliendelea kunitesa moyoni mwangu. Jambo ambalo nilitamani kukuambia kabla halijatokea, ila kutokana nina linda siri za mume wangu pamoja na ndoa yangu isivunjike na kama unavyo ona mwanangu bado ni mdogo na ana hitaji malezi ya wazazi wote wawili”

“Kweli unalo lizungumza. Ehee ni msamaha wa jambo gani unahitaji kuniomba”

Mke wa Mbilinyi akamtazama mwanaye kwa sekunde kadhaa kisha akanitazama na mimi usoni mwangu.

“Ile siku ya harusi yako. Mume wangu alipanga mipango yote ya kuhakikisha kwamba unatekwa na kuuwawa na mzee Mkumbo”

Maneno ya mke wa Mbilinyi yakamstua sana mtoto wake, japo ni mdogo kiumri ila akastuka kidogo na kunitazama usoni mwangu.

“Mama kwa hiyo baba alitaka kumuua baba mdogo Ethan?”

Sote hatuktarajia kupotea swali kama hili kutoka kwa mtoto mdogo kiasi hichi.

“Ahaa hapana hakuhitaji kunai. Itakuwaje rafiki yangu aweze kunai?”

Nilizungumza ili mradi kuto muweka mtoto huyo katika mawazo mabaya. Laiti angekuwa ni mtu mwengine angepandikiza chuki juu ya huyu mtoto, ila kwangu sihitaji iweze kuwa hivyo.

“Kweli ba mdogo?”

“Kweli mama ametania tu. Si unaona hadi sasa hivi nipo hai hapa”

“Nakupenda ba mdogo Ethan”

Mtoto wa Mbilinyi alinikumbatia na kumfanya mama yake kulengwa lengwa na machozi. Dhambi aliyo ifanya baba yake hakika ni kubwa ambayo ina wanastahili wote kufa.

“Shemeji tutazungumza. Il nimelipokea hilo”

“Kweli shemeji?”

“Yaa usijali. Mimi nipo tofauti sana hivyo ninasamehe kama Mungu anavyo wasamehe waja wake”

“Nashukuru sana shemeji”

Mke wa Mbilinyi akanisogelea na kunikumbatia. Nikamkabidhi mwananye kisha nikatoka ndani humu na kuufunga mlango huu kwa nje. Hasira ambayo hakika imenijaa kifuani mwangu inanifanya nijikute nikipiga ngumi ukutani. Nikaingia katika chumba cha Mbilinyi na kukuta Claudia akimnywesha uji.

“Toka humu ndani?”

Nilizungumza kwa sauti nzito iliyo jaa msisitizo Claudia kuweka kibakuli cha uji chini na kutoka ndani humu pasipo kuzungumza jambo lolote.

“Mke wangu na mwanangu wapo wapi?”

“Mke wako kumbe alifahamu juu ya mpango wa kuniua. Kwa nini ulijawa na roho ya kuto kuwa na huruma. Mwanao hadi sasa hivi ana niita baba mdogo, ana upendo wa dhati kwangu na amefurahi kuniona nikiwa hai. Ilikuwaje kwako Mbilinyi?”

Nilizungumza huku machozi yakinilenga lenga usoni mwangu.

“Mwanangu kwa hiyo yupo hai?”

“Ndio yupo hai. Sina roho mabya ya kuua mtu ambaye hajanikosea kwenye maisha yangu”

Mbilinyi machozi yakaanza kumlenga lenga usoni mwake.

“Tazama ulikuwa tumenda kitu kimoja. Nilijitooa maisha yangu kwa ajili ya familia yako pale ulipo niambia kwamba imeshikiliwa na watu wa mzee Mkumbo. Kumbe ulikuwa una nichora na kunikashifu. Ile siku nahisi ilikuwa ni siku ya kunikamata ila walishindwa. Kwa nini unakuwa hivyo Mbilinyi?”

Niliendelea kuzungumza huku machozi yakiendelea kunimwagika.

“Ilifikia hatua kwamba haukuwa mfanyakazi kwangu. Ulikuwa ni kaka na mshauri wangu wa karibu. Kumbe mtu wako ndio adui yako wa karibu. Umeniingiza kwenye dhambi ambayo mamia ya familia za watu watakao angamia na Mkumbo leo wata nililia. Ila nina shukuru Mungu aliniokoa ili leo niweze kushuhudia jambo kama hili nina shukuru sana”

Baada ya kuzungumza maneno haya nikatembea hadi mlangoni ila nikasimama mara baada ya Mbilinyi kuniita kwa upole. Nikamgeukia na kumtazama.

“Ethan natambua nina stahili kuwa kwa hili nililo lifanya. Ila nina kuomba sana uweze kuisamehe familia yangu”

Sikumjibu chochote Mbilinyi zaidi ya kufungua mlango huu na kutoka. Nikakutana na Romani pamoja na Claudi wakiwa tayari wamesha jianda kwa ajili ya kuelekea katika uwanja wa jangwani. Nikatazama saa yangu na kukuta ni saa kumi kasoro.

“Ifikapo saa kumi na moja kamili mara baada ya mgombea kuanz akujinadi ndio muda nitakao lipua hilo bomu”

“Sawa mkuu”

“Hakikisheni kwamba hamjulikani na mtu yoyote”

“Nimekuelewa mkuu”

“Romani hakikisha kwamba muna rudi na Mkumbo hapa. Claudia hakikisha una rudi salama”

Nilizungumza huku nikimtazama Claudia usoni mwake jinsi alivyo vaa kijigauni kifupi kiasi.

“Sawa Ethan”

Baada ya maelekezo wakaondoka hapa nyumbani kwa kupitia gari ndogo na gari la wagonjwa wanatambua ni wapi wameliweka kwa ajili ya kuhakikisha wana mbebe Mzee Mkumbo mara tu baada ya bomu kulipuka.



Nikaelekea sebleni na kumkuta Piyanka akitgazama matangazo ya moyo kwa moja ya kampenzi za mzee Poul Mkumbo. Idadi kubwa sana ya watu wametoka katika kumsikiliza mzee Mkumbo. Mawazo ya kuwaua maelfu ya watu pasipo hatia yoyote, yakaanza kunitawala kichwani mwangu.

“Mbona una mawazo sana?”

Piyanka aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.

“Ninawaza watu hao wote wanakwenda kufa leo”

“Hatuna jinsi Ethan ni lazima tusimamie mpango ulipo la sivyo huko mbele kutakuwa ni kubaya zaidi ya hili ambalo linatokea leo”

Nikatoa simu ndogo ambayo nitatumia katika kulipulia bomu hilo.

“Usiwe na hofu katika hili Ethan. Nilazima tushinde”

“Sawa”

Baada ya kama nusu saa hivi, Romani akanipigia simu akinijulisha kwamba wamefika uwanjani hapo na hakuna mlizi yoyote anaye watilia mashaka. Ethan akatokea hapa sebleni, kutokana mimi na Piyanka tuna mfahamu, hapakuwa na aliye weza kustuka.

“Kuna lolote linalo weza kutoke kuhusiana na kuzuia jambo hili?”

Piyanka alizungumza huku akimtazama Ethan usoni mwake.

“Hapana”

Ethan akajumuika nasi na kuendelea kutazama tukio hili. Ethan galfa akanyanyuka na kuelekea katika chumba alipo Mbilinyi, baada ya dakika moja akatoka naye na kumkalisha kwenye sofa la peke yake hapa sebleni.

“Ethan familia yangu ipo wapi?”

“Utaiona familia yako mara baada ya kumuona mkuu wako uliye kuwa una mtegemea kwa kila jambo akiteketea”

Ethan alimjibu na nikabaki kimya.

“Wewe ni nani hadi unijibu ikiwa swali langu nimemuuliza Ethan”

Ethan hapo hapo akajibadilisha sura yake na kuwa katika sura yanguna mavazi niliyo yavaa. Mbilinyi akabaki akiwa ametokwa na macho huku akikosa hata la kuzungumza.

“Nina imani kwamba umefahamu kwa nini nimekujibu”

Ethan alizungumza kwa sauti yangu kabisa. Ethan akaondoka sebleni hapa na baada ya muda akarudi akiwa na mke wa Mbilinyi ila akiwa amelala usingizi fofofo. Akamlaza mke wa Mbilinyi katika sofa alilo kaa Mbilinyi ambaye mikono yake na miguu yake imefungwa pingu.

“Mke wangu”

Mbilinyi alijaribu kumuita mke wake huku akimtazama.

“Hawezi kukusikia kwa sasa”

“Umemua mke wangu?”

“Hapana, wewe huoni kama kifua chake kina hema”

Tukaendelea kutazama matangazo ya moja kwa moja ya kampeni za mzee Mkumbo. Ukafikia wakati wa mzee Mkumbo kupanda jukwaani kwa ajili ya kuwahutubia wafuasi wake wanao muamini. Macho ya watu wote hapa sebleni yakahamia kwangu. Mbilinyi akabaki akiwa haelewi ni kitu gani ambacho kinaendelea.

“Muda umefika sasa”

Piyanka aliniambia huku akinitazama usoni mwangu. Nikamtazama mzee Mkumbo jinsi alivyo simama na msemaji mkuu wa chama hicho ambaye ana mkaribisha. Mzee Mkumbo akasimama eneo kilipo kipaza sauti na akaanza kuwasalimia wananchi walio fika eneo hili kumsikiliza.

Jinsi wananchi hawa wanavyo mshangili kwa furaha. Nikajikuta nikianza kulengwa lengwa na machozi usoni mwangu.

“Ethan tunakusubiria”

Piyanka aliendelea kusisitiza. Nikashusha pumzi taratibu huku nikitazama simu hii ndogo niliyo ishika. Meseji ikaingia katika simu yangu nyingine, nikaitoa mfukoni na kukutana na meseji ya Romani akiniambia sasa ni wakati wa kulifyatua bomu hilo. Maisha ya maelefu ya watu kwa sasa yapo mikononi mwangu, japo ni maamuzi magumu sana kwenye maisha yangu kuwahi kuyafanya ila sina budi kuhakikisha kwamba ninayafanya.Nikaminya batani ambayo Piyanka alinielekeza na nikaanza kuzihesabu sekunde thelathini huku nikiwa nimeyafumba macho yangu, baada ya sekunde thelathini nikafumbua macho yangu.

Nikaanza kushuhudia watu wakianza kuanguka makundi kwa makundi, hapakuwa na mtu ambaye alibaki amesimama kwa miguu yake miwili. Hakika sumu hii inafanya kazi kwa haraka sana, tukawashuhudia watu wawili wakikimbilia kwenye jukwaa mbalo watu wote nao wameanguka chini akiwemo mzee Mkumbo. Watu hao walio zifunika sura zao kwa vitambaa vyeupe pamoja na Makati meupe nikawatambua kwamba ni Romani na Claudia. Wakambeba mzee Mkumbo na hatukuweza kuwaona wapi walipo mpeleka kwa maana kamera hii inaonyesha eneo la jukwaa.

“Waooo kazi imekwisha”

Piyanka alizungumza kwa furaha sana. Mbilinyi macho yakamtoka hili alilo lishuhudia hakika si yeye pekee ambaye ameshangaa, ila ni dunia nzima itakuwa imeshangaa kutokana na hichI kilicho tokea. Meseji ikaingia kwenye simu yangu, Romani akinijulisha kwamba kazi imefanikiwa na hivi sasa wapo njiani wanakuja na mzee Mkumbo.

Hasira ya kumuangamiaza mzee Mkumbo ikanitawala moyoni mwangu. Nikatamani hata gari wanalo litumia Romani, lipate na lifike hapa kwa haraka sana. Simu yangu ikaita, kwa haraka nikaipokea.

“Mkuu hatuto weza kuja naye hapo nyumbani kama inawezekana nina omba nikifika kwenye eneo ambalo litakauwa salama basi nikufahamishe uweze kuja.”

“Kwa nini unafanya hivyo?”

“Hiyo yote ni kwa ajili ya usalama wako na usalama wa jambo hili”

“Nimekuelewa”

Nikakata simu na kumtazama Ethan.

“Anacho kuambia Romani ni jambo sahihi. Waambie wavivue viatu vyake, kuna device iliyo tegwa kwenye viatu vyeka. Popote aendapo anaonekana”

Ethan alizungumza na nikampigia simu Romani na kueleza juu ya jambo hilo.

“Sawa boss”

Nikakata simu na kumgeukia Mbilinyi.

“Hilo kundi kubwa la watu walio fariki wakimshangilia bosi wako, wote wamekufa kwa ajili yako. Endapo usinge nisaliti basi nina imani kwamba wasinge kufana ina wezekana ningekuwa nimesha malizana na mzee Mkumbo siku nyingi sana.”

“Unataka kuniambia kwamba watu hao wamekufa?”

“Kwani hujanisikia vizuri au? Utaungana na huyo mkuu wako na mutakufa kwa pamoja”

Mbilinyi akaendelea kushangazwa na maamuzi magumu sana ambayo nimeyachukua kuhakikisha kwama nina lipiza kisasi changu.

“Natambua ni eneo gani wanalo elekea. Piyanka utabaki hapa nyumbani ukimuangalia mtoto wa Mbilinyi ndani huko. Tunaondoka na Mbilinyi pamoja na mke wake”

Ethan alizungumza na sote tuliweza kulitekeleza hilo. Tukaingi ndani ya gari tukiwa na Mbilinyi pamoja na mke wake ambaye hadi sasa hivi hajazinduka. Nikaanza kuendesha gari hili huku nikifwata maelekezo ya Ethan. Tukiwa njiani Mbilinyi akanijulisha kwamba wapo katika mji wa Bagamoyo kwenye moja ya jengo la makumbusho lililopo pembezoni mwa mji na mbali kabisa ya mji wa Bagamoyo.

“Leo nahisi ni siku yangu. Siku ya kuweza kumaliza kila kitu kibaya ambacho nilifanyiwa kwenye maisha yangu”

Nilizungumza huku nikiongeza mwendo kasi wa gari langu.

“Ethan natambua kwamba nimekufanyia mabaya ila nina kuomba usiweze kuia familia yangu”

Mbilinyi alizungumza huku akilia.

“Asikuulie familia yako. Ulivyo fikiria kumsaliti ulihisi nini?”

“Natambu mimi ni binadamu, nina mapungufu mengi ndio maana nimezungumza hayo. Familia yangu haina makosa katika hili”

Nikafungulia redio ya gari ili kukatisha mazungumzo haya ya Ethan na Mbilinyi. Taarifa tunazo zisikia kwenye vyombo vya habari ni majonzi makubwa sana juu ya vifo vya watu hao. Tukafika katika jengo tulilo elekezwa na Ethan akajiweka katika mfumo ambao watu wengine hawamuoni zaidi yangu mimi peke yangu. Tukashuka kwenye gari. Romani akanisaidia kumbeba mke Mbilinyi haku nami nikimkokota Mbilinyi hadi ndani ya jengo hili.

Mzee Mkumbo alipo niona akastuka sana. Uso wake wote umejaa damu kwa kupigwa kipigo kikali ambacho nina uhakika kwamba Romani ndio amefanya kitendo hicho.

“Halooo mzee Mkumbo. Ni muda mrefu sasa umepita hatujaonana”

“We…..we….wewe?”

Mzee Mkumbo alibabaika, na kushinda kuzungumza vizuri. Nikasimama mbele ya kiti alicho kalishwa na kufungwa kamba vizuri. Nikachuchumaa huku nikimtazama vizuri, huku naye akiendelea kunitazama vizuri.

“Hivi mtu akifa na kukufua ana itwa nani?”

“Mzimu?”

Romani alinijibu huku akiwa ameshikilia Mbilinyi aliye na pingu miguuni na mikononi mwake.

“Ohoo hivyo mzee baba nina imani kwamba nimekuwa mzimu kwako”

“Imeku..waje kuwaje ukawa hai?”

“Badala ya kujiuliza imekuwaje kuwaje leo umeingia mikononi mwangu. Unauliza ni jinsi gani nilifanikiwa kuwa hai. Una nishangaza sana. Nina imani kwamba leo hii tunakwenda kumaliza kila jambo kati yangu mimi na wewe”

Nilizungumza kwa upole huku nikimtazama mzee Mkumbo usoni mwake.

“Mwanao kumbe alijifanya kama mtu mwema. Mwanamke mwema kwangu kumbe ni shetani mmoja mbaya sana. Hivyo kabla sijakwenda kudili na mwanao nina mambo mawili nahitaji uweze kufanya”

Nilizungumza kwa sauti iliyo jaa upole kana kwamba ninacho kizungumza sikimaanishi kutoka moyoni mwangu.

“Moja nahitaji ukiri dhambi zako mbele ya dunia kwamba, ulihusika na kifo cha wazazi wangu, kifo changu cha bandia pamoja na kifo cha raisi aliye kuwa madarakani bi Tasiana Ramadhani. Ukisha kiri hayo nitakuua kwa mkono wangu”

“Mbili nikamuue mke wako, mwanao kisha na wewe nitakuua. Ikiwezekana wote niwaue mbele yako, hivyo chagua moja kati ya hayo mawili niliyo kueleza”

Mzee Mkumbo akaka kimya huku akinitazama usoni mwangu. Nikamnyooshea mkono Romani na akanikabidhi bastola yake, nikatoa magazine na kuitazama vizuri na kukuta ina risasi zilizo jaaa. Nikairudisha magazine na kuiweka sawa bastola hii. Kabla sijafanya chochote Mbilinyi akanikabidhi kiwambo cha kuzuia risasi. Nikafunga kiwambo hichi na wala sikuhitaji kuumliza mzee Mkumbo swali jengine. Nikampiga risasi mbili katika paja la mgiuu wake wa kushoto na kumfanya aanze kulia sana.

“Hiyo ninakuonyesha kwamba sina huruma na wewe. Ukimya ukizidi zaidi ya dakika mbili kabla ya kutoa jibu, nina hamia kwenye paja la upande wa kulia”

Mzee Mkumbo akaendelea kugugumia kwa maumivu makali ya risasi hizo. Nikaitazama saa yangu ya mkononi huku nikihesabu jinsi mshale wa sekunde hizo jinsi unavyo tembea taratibu.

“Una sekunde kumi zimesali”

“Moja, moja”

“Romani simu yako si ina uwezo mzuri wa kurekodi”

“Ndio”

“Naomba unipatie”

Romani akanikabidhi simu yake. Tukio hili likanikumbusha kipindi tulipo muua kiongozi wa chama pinzani huku kesi hiyo ikibambikwa kwa mzee Mkumbo na kupitia kashfa hiyo ikapelekea chama chake kumpokonya tiketi ya kugombania uraisi. Nikamuweka mzee Mkumbo sehemu ambayo ni nzuri kwa kurekodia jinsi ya kukiri dhambi zake.

“Unaweza kuanza sasa”

Mzee Mkumbi akanitazama kwa sekunde kadhaa kisha akaanza kuzungumza mambo mabaya aliyo yafanya kwa baadhi ya watu ikiwemo familia yangu. Mzee Mkumbo akaendelea kuzungumza jinsi alivyo tumia nguvu ya bunduki kuhakikisha ana muondoa raisi aliye pita madarakani. Mzee Mkumbo akendelea kutaja viongozi ambao alishirikiana nao kwenye mpango huo. Yote yakiwa yanaendelea ni mimi pekee ambaye niliweza kumuona Ethan akiwa pembeni ya mzee Mkumbo huku akiwa amemshikia kisu cha shingoni. Ila watu wengine na wala kwenye hii video ninayo irekodi Ethan haonekani kabisa.

Kwajinsi mzee Mkumbo anavyo tiririka katika kutaja siri zake ambazo hapakuwa na mtu aliye weza kuziona. Kila mtu alibaki amejawa na mshangao akiwemo Mbilinyi na mke wake ambaye tayari amesha zinduka kutoka usingizini.

“Hayo ndio niliyo yafanya na ninaomba Watanzania muweze kunisamehe”

Mzee Mkumbo alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake. Nikamaliza kurekodi video hii na kuiweka simu hii mfukoni mwangu, kwani video hii nina hitaji dunia nzima waweze kuiona. Nikamgeuka mke wa Mbilinyi ambaye muda wote ana lia huku amemkumbatia mume wake.

“Shemeji, tafadhali nina kuomba umsamehe mume wangu”

Mke wa Mbilinyi alizungumza huku akinipigia magoti mbele yangu. Hakutarajia kama atazinduka na kukutana na jambo kama hili.

“Muna kazi moja iliyo salia ambayo Mbilinyi unaweza kunisaidia wewe na mke wako.”

“Shemeji nipo tayari kufanya chochote utakacho niambia nifanye”

“Kweli?”

“Ndio shemeji”

“Nyanyuka mwaya”

Nilizungumza wa sauti ya upole sana huku nikimtazama mke wa Mbilinyi usoni mwake.

“Unaweza kutumia hii bastola?”

Nilimuuliza mke wa Mbilinyi swali lililo washangaza watu wote ndani humu. Akatingisha kichwa akimaanisha kwamba ana uwezo wa kuitumia bastola hii. Nikamkabidhi bastola hii kisha kwa ishara nikamuamrisha aweze kumua mzee Poul Mkumbo ili hata itakapo tokea kufanywa uchunguzi juu ya kifo cha mzee Mkumbo basi alama za vidole ambazo zitapatikana kwenye bastola hii, zitakuwa za mke wa Mkumbo na yeye ndio atakeye beba kesi hii yote.



Mke wa mkumbo mwili mzima ukazidi kumtetemeka kwa woga. Akaishika vizuri bastola hii huku akivuta pumzi nyingi na kuiachia taratibu. Mzee Mkumbo macho yakamtoka, hakuamini kwamba huu sasa unakwenda kuwa mwisho wake. Mkumbo naye macho yake yote yapo kwa mke wake ambaye ana mwagikwa na jasho jingi sana usoni mwake.

“Shemeji ni nafasi ya pekee sasa kuokoa maisha yako. Mpige risasi ya kichwa huyo mzee”

Nilizungumza kwa sauti ya kunong’oneza pembeni kabisa ya sikio lake. Mke wa Mbilinyi akaendelea kumnyooshea bastola mzee Mkumbo ambaye hana ujanja kabisa. Gafla mke wa Mbilinyi akanigeuzia bastola mimi na kuniwekea ya kichwa.

“Mwana haramu wewe, najua utamuua mume wangu na mimi. Sasa tangulia mbele za hak…….”

Kabla mke wa Mbilinyi hajafanya shambulizi lolote kwangu, nikaupiga mkono wake ulio shikilia bastola na ikaangukia pembeni. Nikawahi kuichukua bastola hiyo, huku mtego ambao niliuweka kwa mke wa Mbilinyi ukiwa umefanikiwa kwani yeye ni msaliti na laiti kama nisinge weza kuwahi kuupiga mkono wake basi angenidhuru. Nikamuwekea shemeji bastola ya kichwa na nikampiga risasi moja iliyoto tokea upande wa pili wa kichwa chake na akafariki hapo hapo. Mbilinyi macho yakamtoka huku akishuhudia jinsi damu ya kichwa cha mke wake jinsi inavyo tapakaa katika sakafu ya jengo hili.

“Mke wako amenilazimisha mimi kufanya hivi”

Nilizungumza huku nikimtazama Mbilinyi usoni mwake. Nikamnyooshea bastola hii kwa sekunde kadhaa, kisha nikafyatua risasi nne kifuani mwake na akaanguka chini. Nikamtazama mzee Mkumbo ambaye muda wote ana shangaa jinsi nilivyo jawa na roho ya kuto kuwa na huruma.

“Una lololote la kuniagiza kwenye familia yako?”

Mzee Mkumbo akaka kimya hukumacho yakiwa yamemtoka. Mzee Mkumbo akakosa la kunijibu. Nikamsogelea mzee Mkumbo, kama jinsi alivyo muua baba yangu kwa kumpiga risasi ndivyo jinsi nami nilivyo tekeleza zoezi la kumuangamiza huku nikimpiga risasi karibia nane mwilini mwake na akapoteza maisha hapo hapo.

‘Hiyo bastola mshikishe mke wa Mbilinyi kisha uondoke hapa’

Ethan alizungumza huku pasipo Romani wala Claudia kuweza kusikia chochote. Nikafamshikisha mke wa Mbilinyi bastola hii, na uzuri eneo alilo kaa anaweza kumshambulia mzee Mkumbo na eneo hilo hilo anaweza kumshambulia mume wake. Hivyo hata ikitokea askari wakifanya upelelezi wao basi hakika watatambua kwamba mke wa Mbilinyo ndio muhusika wa tukio hilo.

“Tuondokeni”

“Mkuu kwa nini umeacha bastola hiyo?”

“Kila kitu atakibeba huyo mwanamke marehemu. Tuondokeni”

Tukatoka nje, Romani na Claudia wakaingia kwenye gari lao kisha nami nikaingia kwenye gari langu na tukamuacha Ethan afanye anacho kifahamu yeye mwenyewe. Tukarudi nyumbani na kumkuta Piyanka akiwa amekaa sebleni na mtoto wa Mbilinyi huku wakizungumza mamno mengi. Nikamtazama mtoto huyu aliye anza kunichangamkia kwa furaha sana.

“Mama yupo wapi?”

“Ameondoka na baba”

“Baba amepatikana?”

“Ndio amepatika hivi sasa wameondoka pamoja wamelekea kwenye shuhuli moja. Wakiimaliza watakuja”

Nilizungumza huku moyoni mwangu nikijihisi maumivu makali sana kwani hili jambo nililo lifanya kwa upende mmoja ni jambo zuri ila kwa upande mwengine ni jambo baya sana na endapo mtoto huyu atafahamu kwamba mimi ndio muhusika wa kifo cha wazazi wake ni lazima atahitaji kulipiza kisasi kwangu au kwenye familia yangu ambayo nitakuwa nimeipata.

Simu yangu ikaanza kuita, nikaitoa mfukoni na kuitazama kwa sekunde kadhaa na kukuta ni Hawa ndio anaye nipigia. Nikaondoka sebleni hapa kwa haraka na kuingia chumbani kwangu na kuipokea simu hii.

“Haloo”

“Niambie mume wangu?”

“Salama, eheee niambie”

“Leo asubuhi nimefanikiwa kujifungua salama, mtoto wa kiume”

“What? Are you sure!!?”

Nilizungumza kwa furaha kubwa sana

“Yes baby. Sasa wewe ni baba”

“Ohoo asante Mungu.”

“Nakutumia picha zake sasa hivi whatsapp”

“Naomba unitumie mpenzi wangu”

“Sawa, tena ana fanana na wewe japo ni mchanga bado ila muna fanana”

“Asante sana Hawa. Nakupenda nakupenda mwaaa”

Hakika furaha ikabadilisha hali yote ya kujihisi ni mwenye dhambi kwa kuwaua watu wengi katika siku ya leo. Baada ya kama dakika moja picha nyingi zikaanza kuingia kwenye simu yangu, nikamshuhudia Hawa akiwa amemshikilia mtoto wangu, ambaye kweli nina fanana naye. Romani akaingia ndani humu mara baada ya kusikia makelele ya mimi kushangilia.

“Mkuu kwema”

Nikamkumbatia Romani kwa nguvu sana huku nikiendelea kushangilia, machozi ya furaha yakaanza kunimwagika.

“Nimekuwa baba Romani. Sasa hivi mimi ni baba”

Nilizungumza huku nikimkabidhi Romani simu yangu. Akatazama picha hizi, taratibu nikamshuhudia uso wake ukijawa na tabasamu pana sana. Akayafumba macho yake kwa sekunde kadha akisha akanikumbatia na kunipongeza.

“Mungu ana makusudi yake mkuu”

“Ni kweli asiee, maadui zangu wameangamia na nimi nina pata mtoto.”

“Hongera kwa kweli”

“Asante. Ila hili jambo nina omba libaki siri mimi na wewe”

“Sawa mkuu”

Nikampigia Hawa simu.

“Ndio mume wangu”

“Mpe mtoto jina la ETHAN Jr”

“Kwa nini?”

“Muite tu hilo jina”

“Sawa mume wangu, kutokana umehitaji iwe hivyo, basi itakuwa hivyo.”

“Jambo jengine nina kuomba usimuweke kwenye mitandao ya kijamii hadi pale nitakapo muweka mimi”

“Sawa baba Ethan Jr”

“Hahaaa”

Nikakata simu huku furaha ikiendelea kunitawala.

“Mkuu natambua hivi sasa upo kwenye wakati wa furaha. Ila huyu mtoto unaniruhusu nikamuondoe duniani. Kwa maana anaweza kutuletea shida hapo baadae?”

Nikashusha pumzi huku nikimtazama Romani usoni mwake.

“Mchome sindano ya sumu kisha mwili wake ukatafute sehemu ya kuutupa na ikiwezekana ukatupiwe baharini au sehemu yoyote”

“Sawa mkuu”

Romani akaniacha peke yangu ndani humu. Nikajitupa kitandani huku furaha ikiendelea kuutawala moyo wangu.

“Hongera”

Sauti ya Ethan ikanistua kidogo.

“Asante sana rafiki yangu”

“Nimewajulisha askari juu zile maiti na nimeweka mfumo ambao utaonyesha Mbilinyi na mke wake wameusika katika kifo cha mzee Mkumbo”

“Ninashukuru sana rafiki yangu. Hakika umenipa nguvu ambayo sikutarajia kuweza kuwa nayo”

“Usijali. Umzuie Romani kumuua huyo mtoto. Mimi nitajua wapi kwa kumpeleka”

“Hivi hato weze kunirudia mimi?”

“Hapana, nitafuta kumbukumbu zake zote na hato jua kama yeye amezaliwa Tanzania au alisha wahi kuwa na ndugu au wazazi Tanzania”

“Unampeleka wapi?”

“Ninampeleka nchini Jamaika, kuna familia ina tafuta mtoto wa kulea. Basi ataishi nchini humo kwa maisha yake yote”

“Nashukuru sana”

Nikatoka ndani humu na kumuita Romani, nikamueleza juu ya kusitisha amri niliyo mpatia.

“Kwa nini?”

“Ataondoka usiku huu huyo binti”

“Ataondoka mwenyewe?”

“Hapana, ila ataondoka”

“Sawa mkuu”

Tukapata chakula cha usiku huku taarifa inayo tawala katika vyombo vya habari nchi nzima ni juu ya maelfu ya watu walio fariki katika uwanja wa Jangwani katika kampeni za mzee Poul Mkumbo. Taarifa ya dharura ikaonyeshwa na ikielezea juu ya kufariki kwa mgombea uraisi mzee Mkumbo huku uchunguzi wa awali wa polisi ukidai kwamba kifo hicho kimesababisha na mke wa aliye kuwa mlinzi wa karibu wa mzee Mkumbo bwana Mbilinyi.

“Hatumo kwaenye hii ishu”

Romani alizungumza huku akinitazama usoni.

“Yaa hatumo kesi wanayo wao wenyewe. Hivi huyu binti ame kula?”

“Ndio amekula na hivi sasa yupo chumbani amelala”

Claudia alinijibu kwa sauti ya upole, nikanyanyuka na kuingia katika chumba cha mtoto wa Mbilinyi na kumkuta Ethan akimtazama mtoto huyo.

“Ni muda wa kuondoka naye sasa”

“Sawa, ila nina kuomba uhakikishe hawezi kukumbuka kitu cha aina yoyote.”

“Usijali niamini katika hilo”

Ethan akambebe binti huyu na wakatoweka kwenye upeo wangu wa macho. Nikarudi sebleni na kuendelea kula na watu wote. Baada ya kumaliza kupata chakula hichi cha usiku nikawaleza juu ya mtoto wa Mbilinyi kuondoka nyumbani hapa.

“Sasa nani amemtowesha!!?”

Claudia aliniuliza huku akinitazama kwa mshangao.

“Yule aliye niokoa kwenye ajali ya kufa baharini na kunileta kwenye kile kisiwa ndio huyo aliye ondoka na huyo msichana”

“Ni hivi Romani na Claudia. Ethana ana rafiki yake anaitwa Ethan. Huyo rafiki yake ni jini, nyinyi hamuwezi kumuona ila leo siku nzima mulikuwa naye akihakikisha kwamba mipango yote ina kwenda vizuri. Huyo rafiki yake ndio aliye mlea huyu Ethan toka alivyo kuwa mdogo sana, akiwa na umri kama wa miaka sita au saba. Si ndio Ethan”

“Ndio”

“Hivyo huyo Ethan mwengine ndio anaye mpatia huyu bwana kaka nguvu ya kuweza kulipiza kisasi kwa maadui zake wote. Nahisi hapo mutakuwa mumenielewa?”

“Nimeelewa ila mkuu kumbe siku zote una urafiki na majini?”

“Sio majini ni jini ila ni mtu pia. Mambo mengine sio rahisi kuweza kumueleza mtu akakuelewa na kukuamini. Yanahitaji moyo na uvumilivu pamoa na wakati wake kufika. Naamini sasa ni wakati sahihi kwa nyie kujua hili. Ila sinto pendelea haya mambo yamuhusuyo Ethan muweze kuyatoa nje. Kitakacho wapata, sijui ni nini kwa maana hata kama akiwa yupo mbali sana, ila ana sikia kila kitu tunacho kizungumza”

“Duu sawa mkuu hatuto lizungumza hilo.”

“Nashukuru kusikia hivyo”

***

Baada ya siku kumi na tatu kupita toka kifo vifo vya maelefu ya watu pamoja na mzee Mkumbo kutokea. Siku ya mazishi ya mzee Poul Mkumbo ikawadia. Maelfu ya watu wakazidi kukusanyika katika kiwanja cha taifa kwa ajili ya kuuga mwili wake, kabla ya kusafirishwa kupelekwa mkoani Singida kwa ajili ya mazishi.

“Haito kuwa hatari kwa wewe kuonekana uwanajani hapo?”

Claudia aliniulza mara baada ya kuwaleza kwamba nina hitaji kwenda kwenye msiba huo.

“Nitajibandika ndevu za bandia na hakuna ambaye ata nifahamu”

“Ila mkuu kumbuka ulinzi sasa hivi kwenye hilo eneo ni mkali sana.”

“Yaa nalitambua hilo, ila mimi sio muhalifu hivyo hata wakigundua kwama nipo hai hakuna atakaye nikamata wala kunihoji ni kwa nini nipo hai”

“Je Biyanka akikuona itakuwaje?”

“Huyo ndio mtu wa pekee ambaye nina hitaji kumfwata na aweze kuniona kwamba nipo hai”

“Mkuu!!!”

“Natambua Romani una wasiwasi, ila usijali katika hili. Andaa mazingira ya mimi kwenda nyumbani kwa Qeen na Latifa mara baada ya kutoka uwanjani”

“Sawa mkuu”

“Nahitaji kukulinda Ethan katika hili kwani nina hisia mbaya sana juu ya hili unalo taka kulifanya”

“Usijali Claudia. Wewe ungana na Romani kwenda kuandaa mazingira ya huko nitakapo kuja. Ila kwa sasa nahitaji kuungana na maelfu ya watu ili kuuaga mwili wa mzee Poul Mkumbo”

Mara baara ya kumaliza kuzungumza maneno haya nikatoka sebleni hapa, huku nikiw animevalia nguo nyeusi tupu pamoja na miwani nyeusi. Ndevu za bandia zikiwa zimebadilisha muonekano wangu kabisa. Nikaingia ndani ya gari langu aina ya Range rover na nikaianza safari ya kueleeka uwanaja wa mpira wa taifa, huku lengo langu ni kuhakikisha kwamba nina kutana na Biyanka uso kwa uso.



Katika siku ambazo jiji la Dar es Salaam lina foleni kubwa sana ya magari ni siku ya leo. Nikaendelea kuvumilia hadi nikafanikiwa na mimi kufika katika uwanja wa taifa. Ulinzi ulipo uwanjani hapa hakika ni mkali sana. Nikafanikiwa kupata eneo la maegesho ya gari langu. Nikajiweka vizuri huku nikijitazama kwa mara kwenye kioo kilichomo ndani ya gari hili. Nilipo hakikisha kwamba nipo vizuri na sio rahisi kwa mtu yoyote kuweza kunifahamu nikashuka kwenye hili gari. Nikapanga mstari na kuwa miongoni mwa waombolezaji wanao ingia ndani ya uwanja huu wa mpira. Wadada nilio simama nao pembeni yangu, hapakuwa na hata mmoja aliye weza kunifahamu. Nikapita hadi kwenye moja ya kiti na nikaa, huku kando yangu akiwa amekaa dada wa kiarubu ambaye alikuwa nyuma yangu kipindi tulipo kuwa tuna ingia uwanjani hapa.

“Watu wamejaa”

Dada huyu alizungumza huku akijipepea na kijidaftari kidogo alicho kishika, kwani msongamano wa watu ulio ambatana na jua kali, hakika husababisha joto kali sana.

“Ni kweli”

Nilizungumza huku nikiendelea kutazama jinsi watu wanavyo zidi kuongezeka katika uwanja huu. Tv kubwa iliyopo hapa uwanjani, inaendelea kuonyesha matukio yanavyo zidi kuendelea ndani ya uwanja huu.

‘Leo ni muda wa kuiweka ile video’

Niliisikia sauti ya Ethan akizungumza nami pasipo kuonekana katika eneo hili.

‘Ila video zote nimezihifadhi nyumbani”

‘Nitakwenda kuzichukua sasa hivi’

Ethan alizungumza na baada ya muda kidogo akarudi.

‘Unataka kuzifanyia nini hizo video’

‘Hii inaweza kuonyesha ufirauni wote ambao mzee Mkumbo ameufanya kwenye maisha yake hiyo watu wasijilize lize kinafiki wakihisi kwamba ni mtu mwema kwao’

‘Mmmm!! Sawa fanya unacho kiweza’

‘Wewe kaa usubiri’

Tukaendelea kuvuta vuta muda huku tukisubiria viongozi kadhaa wakiserikali wakiingia, akiwemo aliye kuwa makamu wa raisi wa bi Tasiana Ramadhani ambaye kwa sasa ndio raisi wa muda. Baada ya viongozi wote kuweza kuingia ukimbini hapa, sasa ikafwata familia ya mzee Mkumbo ambayo imeongozana na mwili wa Marehemu.

‘Kila nimekiweka sawa’

Niliisikia saui ya Ethan kwa mara nyingine.

‘Sawa’

Macho yangu muda wote yanamtazama Biyanka ambaye ameshikiliwa kiuno na mume wake. Roho ya wivu ikazidi kunitawala, hasira ya kutamani kuwaangamiza nayo ikazidi kunitafuta. Kitu ambacho kina nishangaza kwenye nafsi yangu ni jinsi ninavyo endelea kuivaa hii pete ya ndoa yangu ikiwa mwanamke ameweza kuniacha kipindi kirefu sana na amesha olewa upya tena hadharani.

‘Ukipata nafasi ya kuonana na Biyanka leo uta fanya nini?’

‘Nitahitaji kuirudisha kampuni yangu, mgodi wangu kisha nitamuacha aishi’

‘Je yeye asipo kuacha uishi utafanyaje?’

‘Nitafanya kama nilivyo fanya kwa mke wa Mbilinyi, kwani nafasi ya kumpa mtu aishi nina itoa mara moja. Ila akinisaliti na kunigeuka basi huwa sina budi zaidi ya kufanya maamuzi magumu ya kuhakikisha kwamba nina muangamiza.’

‘Sawa’

Muendesha shuhuli hii(mc) akamkaribisha mchungaji kuongoza ibaba hii huku akituomba tuweze kusimama sote. Tukatii huku muda mwingi macho yangu nikihakikisha hayampotezi Biyanka katika jukwaa kuu alilo keti. Mchungaji akaanzisha mauombi yaliyo pelekea uwanja mzima kuwa kimya kabisa, baada ya maombi hayo, mchungaji akatuomba tuweze kukaa. Akaanzisha ibada ambayo muda wote ina tusisitizia kwamba mwili wa mwanadamu ni udongo hivyo kama ni udogo basi utarudi mavumbini.

“Kaka”

Binti wa kiarabu niliye kaa pembeni naye alinita na kujikuta nikimgeukia.

“Una amini anacho kizungumza mchungaji?”

“Kwa nini nisiamini, ikiwa watu wote wata zikwa ardhini?”

“Mmmm haya”

Ikabidhi nimtazame dada huyu kwa makini sana kwa maana sijui kama lengo lililo mleta hapa uwanjani ni hili la msiba.

‘Ethan huyu dada ni nani?’

‘Ngoja nitakuambia’

Ethan alizungumza, gafla tv kubwa iliyopo hapa uwanjani, ikaanza kuonyesha mtoto wa kichina jinsi alivyo lala kitandani pasipo kuwa nguo hata moja. Video hii nina kumbuka niliweza kuirekodi nikiwa na vijana wa Mbilinyi. Video hii haikuishia kuonekana kwenye tv hiyo, ila hata watu wenye simu aina ya smartphone nao walianza kuiona video hiyo. Minong’one ikaanza uwanjani hapa huku kila mmoja akijawa na mshangao mkubwa sana. Nikamuona Biyanka akisimama huku macho yamemtoka. Video hii ikazidi kwenda mbali mara baada ya kumuonyesha mzee Mkumbo akitoka bafuni na kufikia kitandani.

“Ohooo!!”

Binti wa pembeni alizungumza mara baada ya kumuona mzee Mkumbo akimla denda binti huyo wa kichina. Mzee Mkumbo bila hata ya uruma akaanza kula tunda la binti hoyo mwenye umri mdogo sana. Walinzi wengi walipo hapa uwanjani wakaanza kujitahidi kulinda jukwaa kuu lililo jaa viongozi ili hata kama kuna mtu yoyote ambaye amekusudia kuwashambulia viongozi hao basi asiweze. Video hii ikaenda hadi mwisho, kisha ikafwata video ya pili ambayo ni wiki kadhaa nyuma niliweza kuirekodi na inamuonyesha mzee Mkumbo jinsi anavyo kiri makosa aliyo yafanya.

“Ninaitwa Poul Thomas Mkumbo. Nina umri wa miaka stini na nne. Nina mke na mtoto wangu wa kike. Biyamka Mkumbo”

Watu wote wakaka kimyahuku kila linalo onekana hapa ni jambo la kustajabisha kwa kweli.

“Mikono yangu ina damu za watu wengi sana. Nimeteka, nimeua na nimetengeneza mipango ambayo iliweza kuwadhulumu wananchi wengi mali zao pamoja na uhai wao.”

“Mgodi wangu uliopo Moshi. Niliuchukua kutoka katika mikono ya mzee mmoja ambaye jina lake silifahamu. Ila jina la kijana wake anaitwa Ethan.”

Miguno ikaanza uwanjani hapa.

“Nilimuua baba yake Ethan huku vijana wangu wakimbaka hadi kufa mke wake. Lilikuwa ni jambo la furaha sana kwangu mara baada ya kugundua kwamba eneo la shamba hilo ambalo lilijaa madini mengi, litakuwa ni la kwangu. Sikujali juu ya kijana mdogo ambaye ni Ethan, niliagiza aweze kuuwawa”

“Jamani kumbe huyu mzee alikuwa katili hivi”

Dada huyu alizungumza huku machozi yakimlenga lenga usoni mwake.

“Nilijipatia pesa nyingi sana kwa ajili ya mgodi huo. Ethan aliweza kukua, na akarudi nchini Tanzania huku nikimtazamia kama mfanya biashara mkubwa sana. Isitoshe aliweza kuingia kwenye familia yangu mara tu alivyo mchumbia mwanangu Biyanka. Kijana huyu alikuwa na lengo moja tu. Kuchukua kila kitu ambacho nilikichukua kwenye familia yake.”

“Ethan Klopp alijitahidi kwa kadri ya uwezo wake kuhakiksha kwamba nina uchukua uongozi wa uraisi, ambao nimetumia pesa nyingi kuhakikisha nina nunua viongozi ndani ya chama changu, wanipatie nafasi ya kuwa mgombea wa chama hicho kwa mara hii ya pili. Kuanzia mwenyekiti wa chama, katibu mkuu na viongozi wengi wa mikoa, niliweza kuwanunua na wote wakawa vibaraka wangu”

Nikashuhudia mama Biyanka akianguka chini na kupoteza fahamu. Jambo hilo lilipelekea walinzi wa kike kuanza kujawa na mishe mishe za kuhakikisha kwamba wana mpa huduma ya kwanza mama Biyanka.

“Nilipo gundua kwamba Ethan sio wangu, mimi na familia yangu tulipanga kumua. Nilimtumia mlinzi wake wa karibu Mbilinyi na aliweza kuwa mpelezi wangu wa kila jambo. Pia mwanangu Biyanka alikuwa ndio kiungo kikubwa sana cha kuhakikisha kwamba tunamuua Ethan Klopp na kuchukua kampuni zake zote anazo zimiliki”

Watu wakaendelea kusikitika kwa maana hili jambo lina umiza kwa kweli. Kwa mtu ambaye mulipanga kumpa dhamana ya kuongoza nchi kumbe ni jambazi mkubwa.

“Mpango wetu ulifanikiwa siku ambayo Ethan aliamua kufunga harusi ya siri na mwanangu Biyanka. Sherehe ilifanyia kwenye boti ambapo nilihakiksha kwamba nina ivamia boti hiyo mimi na watu wangu. Siku hiyo nilimpiga sana Ethan na kumvunja vunja sehemu zake nyingi za mwili. Baada ya hapo boti hiyo tuliizamisha na Ethan Klopp akafia ndani ya boti hiyo.”

Minong’ono ya watu ikazidi kuongezeka.

“Mimi na mwanangu tulichukua kampuni yake ya mawasiliano huku tukiendelea kutafuna nafasi ya kujua mali zake nyingie ili tuweze kufanikisha mpango wa kuwa na pesa nyingi sana za kuchukua madaraka ya nchi hii”

“Mimi ndio niliye muua raisi aliyekuwa madarakani bi Tasiana Ramadhani, huku nikisaidiana na makamu wa raisi wake”

Watu wakaanza kubwatuka, kwani siri imevuja.

“Pia mimi nimehusika katika kuwaua waelfu ya watu siku ya kampeni Jangwani. Lengo likiwa ni kupata huruma ya Watanzania na niweze kupewa kiti cha uraisi pasipo kupingwa”

‘Ethan hapa pamekaaje kwa maana hakukiri hili ile siku’

‘Nilikuambia kila kitu niachie mimi haya ndio matokeo yake’

“Viwanda vyangu vya kusindikia samaki. Vimekuwa ndio eneo kubwa la uingizaji wa madawa ya kulevya kutoka nchi mbalimbali barani Asia. Biashara hiyo ya madawa ya kulevya imeweze kuniingizia kipato kikubwa sana na nina miliki pesa nyingi sana ambazo hata nchi yangu haina uwezo wa kuzimikili”

“Daaa huyu mzee basi tena, ale tu virungu huko Mbinguni”

Dada huyu aliendelea kulaani kwa matendo aliyo yafanya mzee Mkumbo. Nikanyanyuka na kuanza kutoka uwanjani hapa, dada huyu naye akaanza kunifwata kwa nyuma. Nikafika eneo nililo simamisha gari langu na kuingia. Siwezi kutoa gari kwani nyuma yangu kuna magari mengi mengi sana hivyo ina nipasa kusubiri watu walio nyuma yangu, watoe gari zao kisha nami nitoe gari langu. Dada niliye kuwa nimekaa naye pembeni akagonga kwenye kioo cha gari langu huku akiniomba niweze kufungua. Taratibu nikashusha kioo hichi na kumtazama.

“Vipi?”

“Tunaweza kuzungumza kaka yangu kama huto jali”

“Tuzungumze nini?”

“Kama huto jali nakuomba niruhusu kuingia ndani ya gari lako”

‘Ethan huyu ni nani naye?’

‘Ni malaya wa mjini ametokea kukuchunuku’

‘So nifanyaje?’

‘Akili kichwani mwako’

‘Ahaa….sasa haya’

Nikampa ishara azunguke upende wa pili wa gari na aweze kuingia ndani ya gari. Akafanya hivyo na kuingia ndani ya gari.

“Unahitaji nini?”

“Naamini kwamba litakuwa ni jambo la kukushangaza kaka yangu. Ila nisiwe mnafki nimetokea kukupenda sana”

“Utampendaje mtu usiye mfahamu?”

“Sijajua ila moyo wangu umejaa msukumo mkubwa sana juu yako. Nimejaribu kukaa pale, ila akili yangu yote haikuwemo katika msiba huu zaidi, ipo juu yako”

“Ni hilo tu au kuna jengine?”

“Ni hilo tu kaka yangu”

“Unahitaji kiasi gani cha pesa ili uache kunifwata, kwa maana nina mke na sihitaji kupende. Ona hii pete ya ndoa so nina mke”

Dada huyu akastuka mara baada ya kumuonyesha pete hii.

“Umestuka nini?”

“Eheee”

“Umestuka nini?”

“Wewe ni Ethan?”

Kidogo nikastika na mimi mara baada ya kunitambua. Ila nikajikaza na kutingisha kichwa nikimaanisha kwamba mimi sio Ethan.

“No sasa nina anza kupata picha. Hii pete alinipa Biyanka rafiki yangu nikauze mara tu ya msiba wa mama yangu. Alicho nieleza Biyanka kwamba pete hii zipo mbili tu duniani. Moja unayo wewe na nyingine alikuwa nayo yeye.”

Dada huyu alilama huku akinishika mkono wangu na kuitazama vizuri pete hii.

“Sio kweli, pete hizo wanazo watu wengi dunia”

“Hapana kwa Tanzania hakuna mtu anaye weza kumiliki pete ya dola milioni moja. Ila ni wewe pekee ndio uliweza kununua pete hizo”

“Samahani dada nina kuomba ushuke kwenye gari langu. Nahitaji kuondoka”

“Hapana Ethan ninaomba uniambie ukweli. Imekuwaje hadi leo hii umekuwa hai”

“Aisee umetumwa?”

“Hapana, ninakupenda hata kama wewe ni Ethan ila nimekupenda”

“Dada yangu umechanganyikiwa. Ehee”

Nilizungumza kwa ukali sana huku nikimtazama dada huyu wa kiarubu. Japo ni mzuri sana ila hakika ana nikera kwa jinsi anavyo ning’ang’ania.

‘Usiwe mkali huyo binti atakusaidia kumuingiza Biyanka mikononi mwako. Mkubalie na umpe ukweli’

Maneno ya Ethan yakanifanya nikae kimya huku nikimtazama dada huyu jinsi alivyo jawa na imani kubwa ya kuamini kwamba ndio Ethan Klopp.



“Sijachanganyikiwa Ethan ila ninacho kizungumza naomba unielewe”

“Umekuja na usafiri gani?”

“Nimekuja na gari langu, nimeliacha kule”

“Basi nakuomba uweze kwenda kwenye gari lako. Niachie namba yako ya simu nitakutafuta”

Dada Huyu akanitajia namba yake na nikainakili kwenye simu yangu.

“Hakikisha umuambii mtu yoyote kwamba nipo hai”

“Kumbe nimepatia waooooo”

Dada huyu akachanua mikono yake na kunikumbatia kwa nguvu huku akiwa amejawa na furaha kubwa sana. Akataka kunipiga busu la mdomoni ila nikamzuia na akanibusu shavuni. Akashuka kwenye gari huku akiwa na furaha kubwa sana. Ikanilazimu kukaa ndani ya gari hadi pale shuhuli ya kuuga mwili wa mzee Mkumbo ilipo malizika, kwani gari langu lipo katikati ya magari yawatu wengine hivyo imeniwia ugumu kwa mimi kuweza kulitoa eneo hili gari langu.

“Romani nipe ratiba ya maandalizi”

Nilizungumza huku nikiwa nimeishika simu yangu mkononi.

“Unaweza kuja mkuu”

“Umewaambia kwamba nina kuja?”

“Hapana ila nimewaeleza kwamba kuna mgeni maalumu anakuja hivyo wanatakiwa kujiandaa”

“Sawa”

Majira ya saa tisa alasiri nikafika katika nyumba anayo ishi Qeen na Latifa. Romani akanifungulia geti na nikasimamisha gari langu na kushuka.

“Vipi mgonjwa yupo wapi?”

“Yupo chumbani pamoja na nesi wake ambaye ni muangalizi”

“Hali yake ipo vipi?”

“Mmmmm nenda kajionee tu mkuu”

Tukaingia sebleni. Qeen akabaki akiwa amesimama kwa mshangao huku glasi ya juisi aliyo ishika ikimponyoka mkononi mwake. Mshangao huu moja kwa moja nikatambua kwamba hakutarajia kuweza kuniona mimi katika eneo hili.

“Habari yako Qeen”

Nilimsalimia huku nikimfwata sehemu aliyo simama. Machozi taatibu yakaanza kumtiririka usoni mwake. Akaunyanyua mkono wake wa kulia na taratibu akanishika kwenye paji langu la uso na kuanza kunipapa taratibu.

“Ni wewe Ethan?”

“Ndio ni mimi”

Qeen akanikumbatia kwa nguvu na kuanza kuangua kilio kIkunwa hadi nesi aliyekuwa chumbani akatoka na kutazama ni nini kinacho mliza Qeen.

“Latifa ameteseka sana, tafadhali njoo umukoe”

Qeen alizungumza huku akinishika mkono na tukaingia katika chumba alicho lazwa Latifa. Moyo wangu ukajikuta ukipata maumivu makali sana mara baada ya kumuona Latifa. Mwili wake umekondeana, uzuri wa sura yake umepungua kwa kiasi kikubwa sana. Latifa alipo niona taratibu akautupa mdoli alio kuwa ameukumbatia na taratibu akaninyooshea mkono huku akitamani niweze kumshika. Nikamsogelea na kuushika mkono wake, akajaribu kunyanyuka kitandani ili akae, ila akajikuta akishindwa. Hii yote ni kutokana na kudhohofika mwili wake.

Hatukuweza kuzungumza kitu cha aina yoyote zaidi ya kuanza kulia kwa uchungu sana huku tukikumbatiana kwa zaidi ya dakika ishini.

“Ethan”

Latifa aliniita kwa sauti ya chini na iliyo jaa upole wa hali ya juu.

“Mmmm”

“Nakupenda sana mume wangu wangu”

“Nakupenda pia mke wangu”

“Niambie kwamba huto ondoka na kuniacha tena?”

“Siwezi kukuacha mke wangu”

“Apia”

“Haki ya Mungu vile”

Latifa akanikumbatia kwa nguvu sana huku dhairi akionyesha kujawa na furaha.

“Qeen niletee chakula, leo nitakula mimi mwenyewe”

Latifa alizungumza na kumfanya Qeen apanguse machozi yake kisha akatoka ndani humu. Hakika siku ya leo, ni siku mpya kwa Latifa, kwa jinsi alivyo fakamia mtoro huu alio pikiwa hakika kila mtu ambaye alishuhudia siku zote akikataa kula, amebaki akiwa na mshangao. Nikamshuuri Latifa kumpelekea hospitalini ili apate matibabu zaidi, hakuwa na pingamizi la aina yoyote, akakubaliana na kile nilicho mueleza.

Tukampeleka hospitalini na akaanza kupata matibabu mazuri huku akiwa chini ya ungalizi wa madaktari wazuri sana. Baada ya siku mbili za matibabu na kula vyakula vyenye kuujenga mwili wake. Afya ya Latifa ikaanza kubadilika, mifupa ambayo ilijitokeza kutoka na kukonda taratibu ikaanza kupotea.

“Mbona una nitazama sana mume wangu?”

Latifa aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu kwa tabasamu pana sana.

“Napenda kukutazama tu mke wangu”

“Najua sasa hivi nimekuwa mbaya ila nitarudi kwenye hali yangu ya kawaida”

“Mbona ni mzuri. Usijihisi kwamba wewe ni mbaya Latifa”

“Najua nimekonda sana mume, ila nitarudi na kuwa poa”

“Nitahakikisha kwamba hii hali haitokei tena kwenye maisha yako. Sawa”

“Kweli mume wangu?”

“Ndio mke wangu”

Ndani ya wiki moja hali ya Latifa ikarudi katika ubora wake. Tukarudi nyumbani huku mipango ya kuirudisha kampuni yangu ya mawasiliano pamoja na mgodi wa baba yangu ukiwa una endelea chini kwa chini. Pasipo Biyanka kufahamu juu ya uwepo wangu hapa duniani.

“Baby”

“Naam”

“Utamfanya nini Biyanka mara baada ya kurudisha kila kilicho chako?”

“Nahitaji kumfilisi yeye na mama yake. Ila nahitaji kuwatumia nyinyi kuhakikisha kwamba muna rudisha mali zangu zote zilizo potea”

“Kwa mimi nipo tayari mume wangu, tena hata sasa hivi nipo tayari ni wewe tu kunipa njia ambayo inaweza kunifanya turudishe mali zako”

Latifa alizungumza huku akiwa amejawa na furaha sana.

“Tukifika nyumbani tutapanga”

Nilizungumza huku nikeendesha gari langu taratibu. Tukafanikiwa kufika nyumbani salama salamini. Suprize ya sherehe ya kumkaribisha Latifa nyumbani ikatushangaza sisi sote wawili, kwani hata mimi sikutarajia kama Qeen, Romani na Claudia wanaweza kutuandalia sherehe hii.

“Mbona hatuja fahamishana jamani”

“Tungekufahamisha ungemuambia shemeji”

Romani alizungumza kwa furaha. Hakika timu yangu ambayo niliianza nayo kwenye zoezi zima la kulipiza kisasi sasa imerudi japo hapo katikati niliyumba na kuwa na Biyanka ambaye mwishowe alinisaliti.

“Romani nina imani kwamba utakuwa na mpango mpya?”

“Ndio mkuu”

“Basi sherehe ikiisha utanijulisha.”

Sherehe hii ya watu wachache ikapamba moto hadi majira ya saa saba usiku, ambapo mimi na Latifa tukaamua kuingia chumnbani kwa ajili ya kumpumzika. Latifa hakuitaji kunipa nafasi hata ya kupanda kitandani, akanivua jinzi niliyo ivaa na kumshika shika jogoo wangu aliye anza kusimama taratibu.

“Mke wangu kumbuka dokta amesema unatakiwa kupumzika”

“Sio kwa kukumiss huku mume wangu. Nitapumzika siku nyingine”

Latifa taratibu akaanza kumnyonya jogoo wangu, huku mikono yangu ikiwa na kazi ya kukatika kwenye kila kona ya mwili wake. Vilio vya kimahaba vya Latifa vikaanza kutawala ndani ya chumba hichi mara baada ya kuanza kumnyonya kitumbua chake kwa utaalamu ambao, mwanamke yoyote akinyonywa ni lazima atasisimka.

“Fuc** me baby”

Latifa alilalama huku viungo vyote vya mwili wake vikiwa vimelegea kisaswa sawa. Nikasitisha zoezi la kumnyonya na taratibu nikamzamisha jogoo wangu katika kitumbua chake. Mtanange huu, ukaanza kwa kasi ya ajabu. Latifa akazidi kuzungusha kiuno chake mithili ya feni. Hadi tunamaliza mzunguko wa pili, bado kiu yake ya kuhitaji kuendelea na mtanange, imemtawala.

“Ngoja nipumzike kidogo tutaendelea mke wangu”

Nilizungumza huku nikihema sana, kwani nimetumia nguvu na kasi kubwa kuhakikisha kwamba nina mpa Latifa mapenzi moto moto.

“Sawa Ethan wangu. Haki ya Mungu nilikuwa nina umwa kwa kuosa haya mautamu. Yaani nimepizz mara nne na bado nataka…Haaa hapana wewe mwanume mbo** yako ni tamu sana”

“Kweli?”

“Haki ya Mungu, yaani hapa namsubibiria kidogo anyanyuke aendelee kunipa mautamu”

“Hahaa haya mwaya”

Baada ya dakika kumi, Latifa akaanzisha uchokozi wa kumshika shika jogoo wangu, huku uchokozi huo ukizidi kwenda mbali zaidi na akahamia katika shuhuli ya kunyonya. Kama ilivyo kwa mwanaume rijali, akifikia katika hatua hiyo basi ni lazima ahakikishe kwamba ana mpa kipondo kizito mwanamke huyo aliye mchokoza.

Mzunguko huu wa pili hakika haukuwa wa kawaida. Mzunguko huu ninaweza kuufananisha na mpambano wa masumbwi kati ya Tyson na Evander. Latifa hakusika kuning’ata kifuani mara baada ya kuhisi mtandange unakwenda kumuhelemea. Sikulijali hilo, ila nilicho kifanya ni kuongeza mashambulizi hadi Latifa yeye mwenyewe akakiri kwamba nimepiga KO(Knock out).

“Ahaa kum** yangu ina waka moto mume wangu….Huuuuuhuhu uwiiiiiiii”

“Unajisikiaje?”

“Mmm hapana kwa kweli. Toka nikujue Ethan hujawahi kunitomb** hivi”

“Hata mimi sijawahi kutomb** hivi”

“Mmmmm hakika siwezi kukuacha jamani. Yaani umenihamisha, umenipeleka peponi na kunirudisha duniani”

“Haha”

“Yaani hapana kwa kweli. Sitaki kumruhusu kuku yoyote kukuchukua. Yaani nitaua mtu”

Latifa alizungumza sifa nyinngi sana hadi sote wawili tukapitiwa na usingizi. Mlio wa simu yangu ukanikurupusha kitandani, taratibu nikitafuta nilipo iweka, na kuikuta kwenye mfuko wa suruali yangu, niakitoa na kuitazama kwa sekunde kadhaa na kukuta ni Romani ndio anye piga.

“Romani”

Nilizungumza huku nikimtazama Latifa aliye lala pembeni yake, huku kichuguu cha makalio yake kikiwa kimejirocho vizuri.

“Ndio boss. Mupo hai kweli?”

“Hahaa tupo hai habari za asubuhi?”

“Sasa hivi sio asubuhi mkuu. Ni saa saba kasoro”

“Weee”

“Haki ya nani. Tazama saa yako”

Nikatazama saa yangu na kweli ni saa saba kasoro dakika kumi na tisa.

“Aisee sherehe ya jana ndio imetuchelewesha kuamka”

“Ni kweli. Nina habari mpya kabisa na muhimu nahitaji kukuambia”

“Habari gani?”

“Ukiamka nitakuambia”

“Sawa”

Nikakata simu na kuiweka mezani nikajigeuza upande wa pili wa kitanda alipo lala Latifa. Nikamtazama kwa dakika kadhaa huku nikisifu uumbaji wa Mungu kwa huyu mwamake.

‘Mungu fundi’

Nilijikuta nikizungumza kimoyo moyo huku nikishika wowowo la Latifa na kulitingisha kidogo.

“Baby umeamkaje?”

Nilizungumza kwa sauti ya upole kidogo huku nikimtazama Latifa usoni mwake.

“Safa tu mume wangu”

“Amka muda umekwenda sasa.”

“Mmmm naomba kidogo mume wangu”

“Tutafanya kidogo mke wangu. Sasa hivi nahitaji kwenda kuzungumza na Romani”

“Jamani kidogo tu mume wangu. Mmmm!!”

Latifa alizungumza huku akinishika shika jogoo wangu ambaye hakuhitaji kuonyesha udhaifu wa kuto kusimama. Kwajinsi Latifa anavyo nibembeleza ndivyo jinsi nami nilivyo jikuta mzuka ukipanda na nikamuweka sawa Latifa na taratibu nikaanza kumpa, utamu anao stahili kuupata. Baada ya kumaliza mtanange huu, tukaingia bafuni kwa pamoja na kuoga, tukabadilisha nguo na kutoka chumbani hapa. Tukasalimiana na wezetu kisha Romani akaniomba tutoke nje tuweze kuzungumza na nikatii.

“Mkuu kuna habari nzuri na njema”

“Ehee niambie”

“Biyanka amekaribisha wawekezaji katika kuwekeza katika mgodi wa baba yake pamoja na kampuni yake ya simu. Hivyo kutakuwa na mashindano ya kununua hisa, tukifanikiwa kununua hisa nyingi basi tunachukua migodi na kampuni kwa njia ya amani kabisa pasipo kumwaga damu”

Nikajikuta nikitabasamu kwa kweli kwa maana bado sikuwa na njia sahihi ya kuweza kurudisha mali zangu mikononi mwangu ila kutokana njia hii imepatikana basi nitahakikisha nina nunua hisa nyingi sana kuliko watu wote na nitajua jinsi gani nitairudisha pesa yangu hiyo nitakayo wekeza kwenye hisa hizo.



“Katika hili ina bidi wewe uweze kusimama. Kwa maana hatuwezi kumtumia Qeen wala latifa kwenye hii ishu ni rahisi sana kwa wao kuweza kujulikana”

“Hakuna shaka muheshimiwa”

“Romani”

“Naam”

“Naomba uwe unaniita Ethan, usipende kuniita bosi wal Mkuu.”

“Nimekuelewa pia katika hilo”

“Nashukuru. Hembu fwatilia tuhakikishe tunaitumia karata hii kuchukua kila kilicho changu”

“Sawa Ethan”

Mipango na mikakata ya kuzidi kuhakikisha kwamba nitachukua mali zangu ikazidi kupamba moto. Sikuona haja ya kuendelea kujificha katika baadhi ya wakurugenzi wanao simamia makampuni yangu katika nchi Mbalimbali duniani. Kila mmoja aliye tambua juu ya uwepo wangu, akajawa na furaha na matumaini makubwa sana.

“Ni lini mkuu utarudi Ujerumani”

Mkurugenzi wa kampunzi yangu ya magari ya BMW aliniuliza tukiwa tunazungumza kwa kupitia video call.

“Baada ya kumaliza kila kitu. Ila ninashukuru kwa kuendelea kusimamia kampuni yangu”

“Ni jukumu langu mkuu”

“Nashukuru”

Mawasiliano yakaishia hapa. Baada ya siku mbili, siku ya kuanza kununua katika hisa katika kampuni mbili ikaanza. Tukaelekea mkoani Moshi na usafiri wa ndege ya kukodi. Maandali ya magari tutakayo tumiak uelekea migoni, tukakatuka yakiwa yamekamikika kama jinsi vile Romani alivyo panga. Tukafika eneo la migoni huku tukiwa watu wote watano. Romani na Claudia wakashuka kwenye gari huku wakiwa wamependeza na kwa haraka haraka mtu ukiwatazama ni lazima utafahamu ni mtu na mke wake. Wawekezaji mbalimbali nao wakafika migonidi hapa huku kila mmoja aweze kuhakikisha kwamba anakuwa mmiliki mkuu wa mgodi huo.

“Sipati picha Biyanka akigundua kwamba mimi ndio mnunuzi wa hizi mali”

Nilizungumza huu tukiwa tumekaa ndani ya gari.

“Atachanganyikiwa, ila mpenzi wangu unatakiwa ufanye jambo kubwa zaidi ya hili juu ya huyu mwanamke”

“Jambo gani?”

“Hata ikiwezekana kumuua. Ujue amekurudisha nyuma kwa kiasi kidogo”

“Latifa sasa hivi muda wa kumwaga damu. Acha tutumie akili katika hii vita. Si unaona mara ya kwanza tilivyo tumia akili na mambo yakanda fresh tu”

Qeen alijibu kwa maelezo yaliyo jitosheleza.

“Ni kweli unacho zungumza Qeen”

Majira ya saa tano asubuhi, zoezi la kuuza hisa za mgodi huo zikaanza. Makampuni makubwa kutoka bara la ulaya na Asia wakawa na kazi ya kupigana kikumbo na Romani aliye simama yeye kama yeye. Hisa asilimia themanini na tano ambazo zimewekwa sokoni, zikazidi kutoa watu udenda kwa maana ukinunua hisi hizo, moja kwa moja umekuwa mmiliki wa mdodi huo na hao wamiliki wa hisa kumi na tano zilizo salia, hawana nguvu na maamuzi juu yako. Uzuri ni kwamba Romani amevaa kinasa sauti ambacho tunaweza kuwasiliana mimi na yeye moja kwa moja.

“Mkuu imfika dola bilioni moja”

Romani aliomba ushauri mara baada ya muwakilishi wa kampuni ya mafuta kutoka Dubai kutaja kiasi hicho cha pesa.

“Weka moja pointi moja. Wewe nenda nao hadi wewe ndio uwe mmiliki”

“Sawa”

Majibizano ya kupanda bei katika hisa hizi zilizo uzwa kama mnada zikazidi kupanda bei.

“Dola bilioni moja pointi nane”

Mtu mmoja alizungumza.

“Dola bilioni mbili nukta tano”

Romani akavunja kabisa matumaini ya watu wengi waliopo hapo. Hapakuwa na mtu mwengine aliye nyanyua kinywa chake katika kutangaza dau kubwa juu yake. Muongoza mnada huo wa hisa, akafika hatua ya tatu kabisa ya kuwauliza kama kuna mtu atapanda na wote wakaka kimya na kumfanya Romani kuibuka kuwa mshindi.

“Tumefanikiwa mkuu”

“Yaaa hizo pesa wanahiji zilipwe ndani ya wiki moja si ndio?”

“Ndio”

“Sawa tunarudi Dar hakikisha mwendo ndio huu huu. Hakuna kuacha kitu”

“Nimekuelewa Ethan”

Baada ya kuandikishana kwa Romani kwamba ndio msihindi wa mgodi huo. Tukarudi uwanja wa ndege na kurudi jijini Dar es Salaam kujiandaa na mnada mwengine wa siku inayo fwata ambao unahusiana na hisa za kampuni yangu ya mawasiliano ya simu za mkononi.

Siku iliyo fwata tukawahi mapema na asubuhi kufika katika jengo la kampuni yangu. Jengo ambalo katika maisha yangu ya kuishi hapa nchini Dar es Salaam limekuwa ni moja ya eneo nililo kaa kwa muda mrefu sana. Hapakuwa na mfanyakazi wala mtu youote aliye weza kufahamu juu ya uwepo wangu ndani ya hili jengo. Mdada wa hisa salimia tisini ukaanza kufanyika katika ukumbi mkubwa wa kampuni hii. Romani na Claudia wakaingia katika kampuni hiyo nao wakiwa ni miongoni mwa wanunuzi.

“Leo nahitaji kwenda katika ukumbi huo mara tu ya mdada kuisha”

“ETHAN!!”

Latifa alijawa na mshangao mkubwa sana juu ya maamuzi yangu hayo.

“Ndio usiwe na hofo. Siwezi kukaa maisha ya kijificha, ni lazima niweze kutimiza ndoto zangu. Ndoto yangu ya kuwa mchezaji mpira bado ipo pale pale, nasubiria Romani ashinde mdada huo ili wakanione vizuri”

“Mmmmm”

Tukaka ndani ya gari hili hadi Romani alipo fanikiwa kununua kampuni hii kwa dola za kimarekani million mia nane. Nikashuka kwenye gari na moja kwa moja nikaelekea kwenye lifti. Qeen na Latifa nao hawakuhitaji kuniachapeke yangu. Tukapandisha hadi gorofa la mwisho kabisa ulipo ukumbi wa mikutano. Miwani nyeusi niliyo ivaa kidogo ikawafanya baadhi ya wafanyakazi nilio kutana nao kushangaa shanga. Tukaingia ndani ya ukumbi huu huku na watu wote wakatazama mlangoni tulipo ingia sisi. Taratibu nikaanza kutembea hadi eneo la muendesha mnada wa hisa hizi, huku minong’ono ya chini chini ikianza kutawala ndani ya ukumbi huu. Biyanka na mume wake macho yakawatoka kiasi cha kuwafanya wasimame kwenye viti walivyo kalia.

Nikavua miwani hii na kuwafanya watu wote kushangaa, kwani sura yangu halisi imeonekana. Nikaka kimya kwa sekunde kadhaa huku nikimtazama Biyanka ambaye nina mshuhudia akikaa mzima mzima kwenye kiti chake.

“Ninaona kampuni yangu inauzwa ingali bado nipo hai?”

Kamera za waandishi wa habari zikanielekeza mimi, huku kila mmoja akijitahidi kuhakikisha kwamba ana pata picha ambayo itakuwa ni picha nzuri ya kuirusha kwenye chombo chake cha habari.

“Nani aliye idhinisha juu ya kuuzwa kwa kampuni yangu?”

Watu wote wakaa kimya. Biyanka na mume wake wote wakawa kama watu walio mwagiwa maji ya baridi kwani si kwa kupooza huko.

“Muliona haitoshi kunia wewe na baba yako, mumeamua kuuza hadi mali zangu si ndio?”

Niliendelea kuzungumza kwa kujiamini sana.

“Swala la hisa za kampuni hizi kupigwa mdana liishie hapa na kila mmoja anyanyuke na atoke ndani ya kampuni yangu”

Watu wakaanza kusimama na kutoka ukumbini hapa na kuwaacha waandishi wa habari, Biyanka, mumewe na walinzi wake pamoja na Romani na timu yangu.

“Kwamakosa ya baba yako aliyo kiri mbele ya umati wa watu katika msiba wake. Sidhani kama wewe na mama yako mungestahili kuwepo nje mukipunyanga punyanga kama sasa hivi. Mulipwaswa muwe magarezani.”

Nilizungumza huku nikimwafwata Biyanka na mume wake sehemu walipo kaa. Walinzi wao wakawazunguka ili nisiwashike.

“Mwanamke niliye kupenda. Niliye kujali na kukuheshimu kuliko wanawake wengine wote. Leo hii ndio malipo ambayo una nipatia?”

Maneno yangu yakazidi kumwaga machozi Biyanka ambaye amejiinamia chini.

“Nahisi na wewe umekuwa na huyu mwanamke ili tu mufanye janja janja za kumuingiza madarakani mzee Mkumbo, ila leo hayupo tena. Leo amekufa leo hii umemshauri binti yake kuuza mali zangu ili muweze kuondoka nchini hapa Tanzania si ndio?”

Maneno yangu yakazidi kuwafanya waandishi wa habari kuendelea kurekodi kila aina ya tukio ambalo lina endelea katika eneo hili.

“Nipe kila kilicho changu. Na usalama wenu ni kuondoka katika kampuni yangu la sivyo sheria itafwata mkondo”

Nilizungumza kwa ukali huku machozi yakinilenga lenga usoni mwangu. Hapakuwa na mtu aliye jawa na ujasiri wa kunizuia kuzungumza.

Biyanka taratibu akasimama na kupiga magoti chini huku kichwa chake akiwa amekiinamisha chini, nikajikuta nikitabasamu sana kwani hata hili analo lifanya ni uigizaji mbele ya hawa waandishi wa habari.

“Mchukueni mtu wenu na muaondoke naye. Qeen itasha kikao cha wafanyakazi wangu wote hapa ukimbini. Waandishi wa habari nitakuwa na mazungumzo naye mara baada ya kumaliza kikao na wafanyakazi wangu. Nawaomba mutupishe”

Mume wa Biyanka akamnyanyua mke wake wakaongozana na walinzi wao na kutoka ndani humu huku wakiwa wamejawa na aibu kubwa. Waandishi wa habari wakatoka na wafanyakazi wangu wakainagi ndani humu.

“HIi ndio idadi yote ya wafanyakazi?”

Niliuliza huku idadi ya wafanyakazi ikiwa imepungua kwa kiasi kikubwa.

“Ndio mkurugenzi”

Sekretariw angu alinijibu huku macho yake yakiwa yamejawa na uwekundu ambao unadhihirisha muda mchache ulio pita alikuwa akilia sana.

“Wengine wamekwenda wapi?”

“Walipunguzwa kwa kufukuzwa kazi”

“Na nani?”

“Na huyo jamaa aliye muoa aliye kuwa mke wako”

“Pumbavu sana. Kakae”

“Sawa mkurugenzi, ila ninaweza kukumbatia kidogo?”

“Ndio unaweza”

Sekretari wangu akanikumbatia kwa nguvu. Uvumilivu ukamshinda na kuanza kuangua kilio na kunipa jukumu la kuanza kumbembeleza.

“Bosi nilijua umekufa. Niliteseka sana na kuumia. Nilikata tamaa kabisa ya kufanya kazi kwenye kampuni hii ila shida ndio zilizo kuwa zinanifanya niendelee kuwa mfanyakazi wa hii kampuni”

“Pole sana rafiki yangu. Nimerudi kila jambo litakwenda sawa”

“Sawa mkuu”

Nikamuachia sekretari wangu na kusimama eneo lenye kipaza sauti. Nikawatazama wafanyakazi wangu, tukio la nyuso zao kukata tamaa, hakika linanikumbusha siku ambayo nilimuachia Biyanka kampuni na hali niliyo ikuta kipindi kile hii ni mara mbili yake.

“Habari zenu”

“Salama mkurugenzi”

“Poleni kwa mambo kadhaa ambayo yametokea katikati yenu”

“Tunashukuru sana mkurugenzi”

“Natambua kwamba kampuni hii imepitia mambo mengi na magumu ambayo wengi wenu mumeweza kuyashuhudia. Mwanamke ambaye nilimuamini na kumfanya kuwa mke wangu, ila alinisaliti na mwishowe akahitahi kuiuza kampuni yangu. Ila niwaahidi kitu kimoja, nitahakikisha kwamba kila mtu ana rudi kwenye nafasi yake. Nitahakikisha kwamba kila mmoja ana ifanya kazi yake katika ukamilifu mkubwa na amani moyoni mwake.”

“Sekretari wangu utahakikisha kwamba wafanyakazi wote ambao walisimamishwa kazi kutokana na maswala ya unyanyasaji kazini. Warudishwe na kazi iweze kuendelea kama kawaida”

“Sawa mkurugenzi”

“Nipende kuwatoa hofu. Nipo hai japo walipanga kunia na kunipoteza, ila mkono wa mwenyezi Mungu bado upo pamoja nami, japo huko nje watahiaji kuniangamiza kwa kujitokeza hadharani, ila hilo mimi sinto lijali. Nipo kwa ajili ya kupigania watu wangu na mali zangu”

Nilizungumza huku machozi yakinimwagika mashavuni mwangu. Baadhi ya wafanuakazi wangu nao wakashindwa kujizuia kabisa na kujikuta nao wakimwagikwa na machozi.

“Ninawapenda kutoka moyoni mwangu. Nimejifunza kitu kikubwa sana kwenye maisha yangu. Leo nisizungumze maneno mengi sana. Labda nikaribishe maoni mawili au maswali”

Dada mmoja akanyoosha mkono na nikamchagua.

“Kwanza pole sana mkurugenzi wetu. Katika kipindi hichi cha miezi kadhaa karibia mwaka toka uwe nje ya ofisi yako hakia ni wafanyakazi wengi hatujalipwa mishahara pamoja na marupu rupu yetu je hilo mkurugenzi litakuwaje?”

“Sekretari wangu hakikisha kwamba kila mfanyakazi anaye dai kampuni hii, analipwa leo hii hii. Hadi kuna pambazuka kesho sitaki kuona mtu mwenye deni kwenye kampini yangu. Ehee mzee pale”

Mzee mmojaa kasimama.

“Kwanza pole sana mwanangu. Hakika ni mengi sana umepitia japo hatujui ni yapi umepitia ila Mungu ni mkubwa umerejea tena ukiwa na akili mpya hakika hongera sana. Yangu ni hayo mkurugenzi”

“Asante sana baba yangu. Natambua kwambe wengi wenu muna hamu ya kujua ni nini kilicho nipata kwneye kipindi chote cha kusadikika kwamba nime uwawa. Si ndio?”

“Ndio mkurugenzi”

“Basi sekretari wangu andaa mkutano na waandishi wa habari ndani ya ofisi yangu na nyinyi nyote muweze kutazama mahojiano hayo moja kwa moja kwenye televishion. Nahitaji kuifahamisha dunia nzima kwamba nipo hai na pia nitaomba radhi familia zote zilizo poteza uhai wa ndugu zao kwa ajili yangu.”

Maneno yangu yakamfanya Romani kustuka sana huku akinitazama usoni mwangu kwani endapo nitatoa siri kwamba mimi ndio nimehusika na kuwaua watu walio fariki kwenye uwanja wa Jangwani basi kitakacho fwata hapo ni mimi kuhukumiwa na mahakama.



ENDELEA

Wafanyakazi wangu wakanielewa. Baada ya wafanyakazi wangu kuanza kutawanyika, Romani akanifwata kwa haraka na kunivuta pembeni.

“Ethan usitake kuaniambia kwamba kwenye huo msamaha unataka kuhusisha swala zima la wewe kuzungumzia juu ya watu walio fariki Jangwani”

“Siwezi kufanya ujinga kama huo. Nahitaji kuwaomba msamaha wale walio tangaziwa kwamba nimekufa na wengine waliweza kufa kwa ajili ya mstuko huo”

“Ahaaa…Hapo nimekuelewa”

“Jela kubaya ndugu yangu”

“Ni kweli. Hapo nimekuelewa Ethan”

Tukaelekea ofisini kwangu na kukuta maandalizi ya kuzungumza na waandishi wa habari yakiendelea.

“Ethan”

Latifa aliniita na tukasogea pembeni sehemu ambayo mazungumzo yetu hayato weze kusikiwa na mtu yoyote.

“Kwa nini umemuacha yule mwanamke ameondoka, si ungeita polisi wamkamate?”

“Hapana”

“Kwa nini hapana. Tambua atakwenda kujipanga na kama si kujipanga basi anaweza kutorokea nje ya nchi”

“Hilo nimelifikiria kabisa. Ila ngoja nizungumze kwanza na waandishi wa habari kisha baada ya hapo tutalizungumzia swala lake sawa”

“Sawa mume wangu ila haya zungumza nao”

Nikamtazama Latifa kwa sekunde kadhaa kisha nikampiga busu la shavuni. Nikakaa kwenye kiti changu ambacho ni muda mwingi sana sikuweza kukaa katika hichi kiti. Waandishi wa habari wakaendelea kujipanga ili kila mtu aweze kupata habari itakayo kwenda kuuza katika chombo chake cha habari.

“Jamani mupo tayari?”“Sekretari wangu alizungumza huku akiwatazama waandishi hawa wa habari.

“Ndio”

“Tunaweza kuanza ehee?”

Niliwauliza waandishi wa habari na wote akakiri kwamba wapo tayari.

“Nina inamani kwamba hii ndio mara yangu ya kwanza kuonekana kwenye vyombo vya habari toka kuenea kwa habari kwamba nimefariki dunia kwenye ajali ya boti miezi kadhaa iliyo pita.”

“Aliyekuwa baba yangu mkwe kwa kipindi hicho ambaye kwa sasa ni marehemu mzee Poul Mkumbo. Akishirikiana na walinzi wangu wa karibu waliamua kuniteka siku ya harusi yangu”

Nikaka kimya kwa sekunde kadhaa huku nikisikilizia jinsi kamera za waandishi wa habari jinsi zinavyo endelea kupiga picha huku wengine wakiendelea kunirekodi.

“Naikumbuka siku hiyo, nilipanga kumfanyia mchumba wangu suprize ya kufunga naye ndoa ya siri. Hivyo niliweza kumshirikisha mlinzi wangu wa karibu kabisa kwa kipindi hicho. Anaitwa Mbilinyi, tuliweza kuanda mazingira mazuri ya kuhakikisha kwamba ndoa hiyo inakwenda kufungwa kwa usiri wa hali ya juu. Ni kweli zoezi lile lilikamilika kwa asilimia tisini na tisa pointi tisa”

“Kumbe mtu ambaye nilimuamini sana, kumbe ndio msaliti wangu. Nina imani kwamba nyinyi mutakuwa munajiuliza ni kwa nini baba yangu mke alikuwa ni adui yangu?”

“Miaka kumi na sita iliyo pita, kipindi ambacho nilikuwa na umri wa miaka kama nane hivi kama si saba. Baba yangu aliweza kugundua kwenye shamba lake la kuna madini mengi sana. Kutokana na umasikini wa akili wa baab yangu, aliamua kumshirikisha mwenzake. Ambaye hakuwa muaminifu kwani aliweza kumleta mzee Mkumbo, ambaye hakuona haja ya kuzungumza na baba yangu na kitu alicho kifanya ni kuamua kumuua baba yangu kwa kumpiga risasi ya kichwa. Mama yangu alibakwa na vijana wake mbele yangu huku mimi wakipiga na kwenda kunitupa kwenye bonde kubwa sana ambalo lina mawe mawe mengi sana pamoja mto mkubwa sana kwa chini.”

Nikaona sura za watu jinsi zilivyo jawa na simanzi sana.

“Kichwa changu kiligonga kwenye moja ya jabali na nilipoteza fahamu. Nilipo kuja kuzinduka ndipo nikipo kutana na wazazi wangu walezi ambao ni mzee Klopp pamoja na mke wake bi Jane Klopp. Walinichukua na kunipeleka nchini Ujerumani huku kumbukumbu zangu za maisha yangu ya nyuma zikifutika kabisa kichwani mwangu”

“Ila baada ya miaka kadhaa, niliweza kujijua mimi ni nani, kumbukumbu za miaka ya nyuma zilirudi kichwani mara tu nilipo muona mzee Mkumbo kwenye televishion. Nilijisikia vibaya sana kuona mtu ambaye ameniulia wazazi wangu anagombania kuwa raisi wa hii nchi.”

Nikaka kimya huku nikimtazama Latifa na watu wengine humu ndani.

“Nikasema inanipasa kuhakikisha kwamba nina zuia hilo jambo. Ila kwa kutumia akili nyingi sana. Nilihakikisha kwamba ninaingia kwenye famili ya mzee Mkumbo bila ya yeye kunijua na kweli nilifanikiwa kuingia kwenye familia yake na nikawa mkwe wake. Japo nilimpa ushirikiano mwingi kwenye kwenye kampeni zake ila kwa upande wa pili nilimuandaa bi Tasiana Ramadhani kuwa raisi wa hii nchi. Ni kweli Watanzania waliweza kumpigia kura nyingi mwana mama huyo na akaichukua nchi”

“Mzee Mkumbo alipo gundua hayo, akaona isiwe shida, akaamua kunishambulia kwa risasi siku ambayo nilikuwa nina toka hapa ofisini kwangu. Kama munakumbuka ile habari iliweza kuchukua vichwa vya habari vya vyombo vingi sana hapa Tanzania. Aliye kuwa mchumba wangu kwa kipindi hicho, Biyanka mtoto wa mzee Klopp aliamua kunipeleka nchini Afrika kusini baada ya kupata mstuko wa moyo.”

“Kwakitendo hicho ni kweli nilimuamini yule mwanamke na alizidi kwenda mbali zaidi, kwani alifunga na kuomba kwa ajili ya kupona kwangu. Kumbe kufanya hayo yote alikuwa akihitaji kufahamu ni wapi zilipo mali zangu”

“Walicheza mchazo mbaya yeye na baba yake na siku ya harusi yetu ndipo walipo pata nafasi ya kuniangamiza. Mzee Klopp alinipiga sana na kunivunja baadhi ya viungo vya mwili. Alinifunga kwa pingu mikono yangu na kuiambatanisha na kitanda cha chuma ambacho kilikuwa ndani ya chumba cha boti hiyo.”

“Boti ile ilianza kuzama na kweli, nilifanya kila nililo weza kujiokoa. Nilishindwa kutokana na kupigwa sana na nilipoteza fahamu. Nilipo kuja kuzinduka nilijikuta kwenye kisiwa kimoja ambacho katika kisiwa hicho anaishi dada mmoja ambaye anaitwa Claudia”

“Iliniuma sana nilipo sikia kwamba raisi Tasiana Ramadhani ameuwawa na wananchi wapo kwenye mpango wa kupiga kura ili kumchagua raisi mwengine.”

“Nilitamani kurudi nchini Tanzania ili kujiweka wazi mbele ya watu, ila nilishindwa kutokana na kukosa usafiri wa kutoka kisiwani hapo. Baada ya wiki kadhaa nikiwa kisiwani nikasikia juu ya mauaji ya kinyama katika uwanja wa jangwani. Na mwisho nikasikia kifo cha mzee Mkumbo, kimesababishwa na mke wa aliye kuwa mlinzi wangu, bwana Mkumbo. Hakika kusema kweli nina waomba sana msamaha wananchi walio ondokewa na ndugu zao kwa ajili ya mstuko wa kifo changu. Pia nitatoa kiasi cha dola za kimarekani milioni mia moja kugawa kwenye kila familia iliyo ondokewa na ndugu zao pale jangwani na wengine walio ondokewa na ndugu zao baada ya kusikia kifo changu”

“Nakaribisha maswali”

Waanindishi karibia wote wakaonyoosha mikono yao.

“Ndio kaka hapo”

“Kwanza pole bwana Ethan. Je ni kwa nini umeamua kumuachia huru Biyanka na mume wake ikiwa katika maelezo inaeleza naye ni msaliti kwenye maisha yako?”

“Mimi ni binadamu niliye umbwa na moyo wa kusamehe. Hata ikitokea kwamba moyoni mwangu nime jawa na kinyongo huwa ninaupa moyo wangu nafasi ya kukumbuka yale mambo mema ambayo mtu huyo aliweza kunifanyia. Sihoni sababu ya mimi kumuhukumu Biyanka, ila nilicho kihitaji ni mali zangu tu zirudi mikononi mwangu. Kampuni hii pamoja na mgodi basi”

Baada ya kujibu swali hilo nikamchagua dada mwengine.

“Bwana Ethan, endapo Biyanka akikataa kurudisha mali zako itauwaje?”

“Uzuri kila kitu kipo wazi sasa. Nitaiachia sheria kufanya kazi yake”

“Bwana Ethan je umejisikiaje juu ya kifo cha adui yako”

Nikaka kimya kwa sekunde kadhaa, nikimtazama mtazamaji huyo aliye niuliza swali hilo.

“Huzuni. Mzee Mkumbo kuna kipindi alinipenda kama baba kabla ya kujua kwamba mimi ni mtoto wa mtu aliye muua. Alinishauri mengi na kuniamini kwenye mambo mengi. Hivyo kama vile nilivyo sema pale awali, moyoni mwangu huwa nina kumbuka mema ya mtu ambayo ananifanyia kwenye maisha yangu. Hivyo nimesikitika japo nilihitaji sheria ndio imuhukumu ila mke wa Mbilinyi amechukua maamuzi mkononi”

“Kwamfano askari sasa hivi wakihitaji kukuhoji juu ya kifo cha mzee Mkumbo na mlinzi wako wa karibu. Utawajibu nini ikiwa wewe umedai kwamba ni ulikuwa ni adui yake na alikuulia wazazi wako?”

“Kusema kwamba ni adui yangu sio kwamba nilihusika katika kumuua. Hapana, Polisi wakihitaji kunihoji, nawakairbisha waweze kunihoji ila ushahidi wa video na matukio mabaya aliyo yafanya mzee huyo yapo hivyo hakuna namna ya wao kunihoji”

“Bwana Ethan huoni kama hapo watakuwa wamekuhisi kwamba wewe ndio ulimuagiza mke wa Mbilinyi kwenda kumuua mzee Mkumbo pamoja na mume wake?”

“Ni ajabu sana kwa mtu wa pembeni kutoa oder ya kumua mke wako au mume wako kisha nawe ukajiua. Laiti kama kungekuwa na maslahi yoyote ameahidiwa hapo sawa. Ila kutokana alifanya kwa maamuzi yake yeye mwenyewe, hapo sihusiki kabisa”

“Bwana Ethan mimi ni Khadija ni mtangazaji wa bbc Swahili. Je bado una ndoto ya kurudi kiwanjani?”

“Ndoto ipo na mwaka jana kuna club kubwa duniani ilifanya mahojiano na mimi. Hivyo nasubiri msimu huu uishe kisha msimu ujao nitakuwa mchezaji wa clab hiyo”

“Swali langu jengine bwana Ethan. Kuna picha zilizagaa mitandaoni siku ya jana zikionyesha aliyekuwa mpenzi wako, mtoto wa raisi wa Ujerumani ambaye ni Camila, amefunga ndoa na tajiri wa kimarekani bwana Gate Thomas, je unalizungumziaje hilo swala?”

Habari hii kidogo ikanistua kwa maana sikupata nafasi ya kuiona.

“Ndio nina isikia kwako hii habari”

“Ushahidi wa picha huu hapa”

Mtangazaji huyu akanikabidhi simu yake na nikaanza kuzikagua picha hizo moja baada ya nyingine. Upendo ni upendo, nikahisi maumivu makali sana kwenye moyo wangu, wivu mwingi ukanitawala. Ila nikatengeneza tabasamu la kinafki ili mradi waandishi wa habari wasijue jinsi nilivyo umia.

“Hongera kwao. Ana haki ya kuolewa kwa maana hana taarifa za mimi kuwa hai”

“Je unazungumziaje ndoa ya Biyanka na mume wake mpya?”

“Sina maoni juu ya ndoa yao. Naamini maswali yaishie hapo. Tutatoa utaratibu juu ya jinsi gani tutazigawa pesa hizo kwenye familia zilizo ondokewa na wapendwa wao. Ninawashukuru sana na siku njema”

Nikanyanyuka na kutoka ofisini hapa huku waandishi wa habari wakiendelea kunipiga picha. Tukafika kwenye lifti ikamlazimu Romani kuwazuia waandishi wa habari, tukaingia kwenye litfi hii watu watano na taratibu ikaanza kuelekea chini.

“Ethan kiasi unacho kitoa mbona ni kikubwa sana”

Qeen aliniuliza huku akinitazama.

“Hapana kuna tosha, itakuwa ni oganaziation itakayo shuhulika na dunia nzima”

“Sawa”

Tukafika eneo la chini ambalo ni eneo la maegesho ya magari. Kabla hatujaingia kwenye gari letu. Gari nne nyeusi zilizo andikwa kwa maandishi makubwa meupe POLISI, zikasimama mbele yetu na wakashuka askari walio valia nguo nyeusi huku wakiwa na bunduki mikoni mwao. Mama mmoja mrefu na mweusi, aliye valia suti nyeusi na iliyo mkaa viziri mwilini mwake, akasimama mbele yetu na kutua kitambulisho chake. Kitambulisho chake kinaonyesha kwamba ametoka kitengo cha usalama wa taifa.

“Bwana Ethan Klopp fwatana nasi kwa mahojiano zaidi”

“Munakuja kumkamata bosi wangu kama mualifu au kuomba kuzungumza naye?”

Romani alizungumza huku akiwa amesimama mbele yangu.

“Kijana hili jambo halikuhusu. Kaa pembeni tunaye muhitaji ni Ethan na si wewe”

“Ila ni bosi wangu”

Mama huyu akamta Romani kibao. Romani akataka kuchomoa bastola ila nikawahi kumshika.

“Tulia, nahitaji kuona vitambulisho vya hao watu mulio kua kunichukua”

“Ethan hatujali wewe ni maarufu kiasi gani, una utajiri kiasi gani. Tupo kazini, ingia ndani ya gari”

Mama huyu alizungumza kwa ukali sana, kiasi cha kunifanya nizidi kushangaa. Kundi la waandishi wa habari likatika kwenye lifti ambayo tumejia. Waandishi habari hawakusita kutusogelea sehemu hii tuliyopo huku wakiendelea kupiga picha nyingi.

“Ingia ndani ya gari bwana Ethan”

Mwana mama huyu alizungumza huku akichomoa bastola na kuninyooshea kwenye paji la uso na kuwafanya watu wote kushangaa.

“Hakikisha kwamba muna fwatilia nina polekwa”

“Sawa bosi”

“Ole wake mufwatilie. Nanyi mutajumuika na huyu”

Mwana mama huyu alizungumza kwa kujiamini. Nikaongozana nao na kuongia katika gari la katikati. Pembeni yangu akaka mwana mama huyu huku upande mwengine akika jamaa aliye jazia misuli yake. Wakanifunga pingu za mikononi mwangu na gafla wakanivisha kigunia cheusi ambacho kinanifanya nishindwe kufahamu ni wapi ninapo pelekewa.

“Kunifanya hivi ni sawa na kunichukulia kwamba mimi ni muhalifu"

Nilizungumza kwa kujitetea.

“Tulia panya wewe”

Mwana mama huyo aliendelea kulalama.

“Nyinyi ni kina nani?”

“Nina imani kwamba Biyanka atakwenda kukuua kama ulivyo muua baba yake.”

Maneno ya mwana mama huyu yakanistua sana na baada ya sekunde kadhaa nikahisi kitu chenye ncha kali ambacho moja kwa moja nikagundua ni sindano, kikizama shongoni mwangu. Maji maji ya dawa waliyo yasukuma shingoni mwangu, taratibu yakaanza kunifanya nikose nguvu huku usingizi mkali ukininyemelea na ndani ya sekunde kadhaa nikajikuta nikilala fofofo.



Sauti za mazungumzo ya hapa na pale zikaanza kupenya masikioni mwangu taratibu. Nikajaribu kufutazama ni wapi ni lipo ila sikuweza kugundua ni wapi ni lipo hii yote ni kutokana na kigunia ambacho nimevalishwa kichwani mwangu. Nikajitahidi sana kusikiliza mazungumzo ya watu hao ila sikuweza nifanikiwa kusikia kiti chochote kwani sauti zao zinaonyesha wamekaa mbali nami.

‘Ethan Ethan’

Nilimuita Ethan ila hakuweza kuitikia. Gafla nikavuliwa kigunia hichi na mwanga mkali sana wa taa ya rangi nyeupe ukanipiga machoni hivyo hata mtu ambaye amenifunua kigunia hichi sijaweza kumuona. Nikasikia mlango ukifungwa kwa nguvu huku ukimya ukiendelea kunipiga machoni mwangu.

“Wewe ndio uliye muua mzee Poul Mkumbo”

Niliisikia sauti ya kiume ikitoke nyuma ya taa hii inayo endelea kunimulika machoni mwangu.

“Wewe ni nani unaye nihoji hilo?”

Mtu huyu hakujibu swali langu.

“Wewe ndio umemua mzee Poul Mkumbo”

“Hapana”

“Wewe ndio umemua”

“Utanilazimishaje kujibu kitu ambacho sijakifanya na isitoshe hapa nilipo sitambui kwamba ni wapi ni lipo”

“Hilo la kutambua ni wapi ulipo halikuhusu sawa”

“Kama mupo sehemu ambayo munahitaji kunihoji nahitaji mwanasheria wangu”

“Hapa hakuna cha mwanasheria wala nani? Lazima useme ni nani amehusika na kifo cha mzee Poul Mkumbo”

Nikakaa kimya huku nikishusha pumzi nyingi. Kitu ambacho kinanishinda ni kusimama kwani miguu yangu na mikono yangu imefungwa pamoja na kiti hichi. Taa hii ikazimwa na nikaweza kumuona mwanaume mrefu aliye valia suti nyeusi huku rangi ya mwili wake nayo ikiwa ni nyeusi mithili ya hiyo suti yake. Ndani ya chumba hichi kuna video kamera tatu zilizo simamishwa kwenye kona tatu za chumba hichi na zote zinarokodi kila kitu kinacho endelea katika chumba hichi. Hapa ndipo nikapata uhakika kwamba watu walio nikamata ni wapelelezi ambao wanahitaji kunihoji.

“Watu walio hudhuria katika mkutano wa kisiasi wa mzee Poul Mkumbo. Waliuwawa kwa sumu kali sana ambayo wewe tunahisi kwamba una husika na jambo hilo”

“Una hisi ila huna uhakika si ndio?”

“Una husika?”

“Sihusiki. Ngoja nikuambie kitu kimoja bwana mpelelezi. Huwezi kutengeneza mazingira ya kuhisi kwamba mimi ndio muhusika. Nahitaji mwana sheria wangu aletwe hapa”

Mwanaume huyu akanisogelea na kunitazama kwa umakini usoni mwake. Akafanya ishara moja na watu wawili walio valia makoti meupe wakaingia huku mmoja wao akiwa ni mwanamke na mkononi mwake akiwa ameshika brufcase. Akaiweka mezani kisha wakaifungua, katika brufcase hii kuna sindano pamoja na vichupa vya dawa sita.

Daktari mmoja akanishika mkono wangu wa kulia na kuanza kuupaka paka dawa, jambo ambalo hakika likanifanya nianze kuogopa sana.

“Munanifanyia nini?”

Hawakunijibu kitu chochote zaidi ya daktari mmoja kuanza kunichoma sindano hiyo ambayo toka nizaliwe sijawahi kuhisi mamumivu makali ya mwili mzima kama haya. Sindano hii inafanya nihisi misuli yangu ikivutana sehemu moja.

“Umehusika na mauaji ya mzee Poul Mkumbo pamoja na watu wote walio hudhuria katika mkutao wake wa kisiasa? Usipo zungumza ukweli hakika utaendelea kufa kuteseka na maumivu haya”

Mwanaume huyu alizungumza na kunifanya nizidi kutesaka na maumivu haya. Kila jinsi daktari anavyo isukuma dawa iliyomo ndani ya sindano hii ndivyo jinsi ninavyo jikuta nikitesaka na maumivu haya. Ni bora kufa na maumivu haya kuliko kukiri kwamba mimi ndio nimehusika na kifo cha mzee Poul Mkumbo pamoja na wafuasi wake, kwani kwa kukiri huko nitajikuta nikiingia kwenye matatizo makubwa sana ambayo yatazima ndoto zangu zote.

Mateso ya sindano hizi kali yakaendelea kwa zaidi ya dakika arobaini ila sikuweza kuzungumza kitu chochote zaidi ya kuendelea kusimamia msimamo wangu kwamba sifahamu. Akaingia mwana mama ambaye alikuja kunikamata kipindi nilipo kuwa ninatoka kwenye kikao na waandishi wa habari.

“Mumepata nini?”

“Hatujapata chochote mkuu”

“Muongezeeni sindano”

“Ila mkuu tukiendelea kumchoma sindano hizi atapoteza uhai kwani tayari tumesha mchoma sindano nyingi sana.”

Daktari alishauri huku akimtazama mwanamama huyu.

“Mchomeni nyingine ni lazima akiri”

Mwanamama huyu alizungumza kwa jazba kubwa hadi wafanyazi wake wakabaki wakiwa wamejawa na mshangao mkumbwa sana.

“Samahani mkuu by my professional siwezi kuendelea kumchoma kiasi kingine cha sindano hizi tulizo mchoma tayaari tumevuka kiwango kinacho takiwa kumchoma.”

“Professional professional kitu gani toka hapa”

Mwana mama huyu alizungumza kwa hasira na kumpokonya daktari huyu sindano, akavuta kiasi kikubwa cha dawa katika moja ya kichuoa kidogo kisha akanikita nayo mkononi jambo lililo nifanya nipige kelele kwani dawa hii anaisukuma kwa kasi sana. Maumivu hata ya sindano ya kistapen ni marakumi ya maumivu ya sindano hii.

“Kwa nini unafanya hivi?”

Nilimuuliza mwana mama huyu kwa sauti ya kumnong’oneza huku nikihisi kizunguzungu kikali sana. Mwanamama huyu hakujali chochote, kizunguzungu kilocho changanyikana na maumivu makali sana, kinifanya nipoteze fahamu.

***

Ubaridi mkali ukanifanya nizidunke usingizini. Nikajikita nikiwa nimelala katika sakafu iliyo mwagwa barafu nyingi huku mwilini mwangu nikiwa na boksa tu. Nikajaribu kuangaza kila kona ya hichi chumba ila sikuona mtu yoyote zaidi ya mlango ulio fungwa. Baridi kali iliyomo kwenye chumba hichi hakika ni kali sana, nikajaribu kupiga hatua moja mbele, miguu yangu ninahisi kama imefungwa mawe mazito sana japo hayaonekani mawe hayo.

‘Lazima watalipa katika hili’

Nilizungumza kimoyo moyo huku sura ya yule mwama mama aliye nifanyia ukatili mkubwa sana ikiwa inanirudia rudia kichwani mwangu. Wakaingia watu wawili walio valia nguo nyeusi wakanishika mikono yangu yote miwili kisha wakaanza kuniburuta na wakanitoa nje ya chumba hichi. Nikaingizwa kwenye chumba nilicho tolewa mara ya kwanza huku nikiwa na boksa yangu. Macho yangu yakagongana na mwana mama ambaye ananichukia kuliko kitu chochote.

“Mfungeni shoti”

Mwanamam huyu aliwaamrisha watu hao. Wakanikalisha katika kiti na kukifunga na pingu. Wakanibana vidole gumba kwa vibanio viwili vya umeme.

“Nakuuliza kwa mara ya mwisho. Wewe ndio uliye husika na kifo cha mzee Mkumbo pamoja na halaiki ya watu ambao waliudhuria katika mkutano wake wa kisiasa”

“Niue ila ukweli ni kwamba sijafanya kosa kama hilo. Hivi ni kwa nini musimuhukumu mzee Mkumbo baada ya kukiri kila jambo baya alilo lifanya kwa watu. Eheee?”

“Usitufundishe. Washa ataeleza”

Kijanawake mmoja akawasha shoti hii ya umeme ambayo imeanza kunipiga kuanzia miguuni hadi kichwani na kunifanya nitetemeke kwa maumivu makali sana.

‘Ethan mbona una acha ninateseka sana hivi?’

Niliwaza kwenye ufahamu wangu wa akili huku nikiendelea kupata mateso haya ambayo ni magumu sana kwenye maisha yangu. Gafla taa zote ndani humu zikazimika, hata zoezi la mimi kupigwa shoti likasimama. Milio ya risasi ikaanza kusikika.

“Hakikisheni mfungwa hatoweki”

Mwana mama huyo aliwaamrisha vijana wake ambao hatuonani kabisa, kwani giza lililomo ndani ya chumba hichi ni kubwa sana.

“Sawa mkuu”

Milio ya risasi ikazidi kujongea katika chumba tulichopo. Mlango wa chumba hichi ukafunguliwa na miale myembaba yenye rangi nyekundu ikaonekana ikikatiza katiza ndani ya chumba hichi na hapa nikasikia vizuri milio hiyo ya risasi huku ikiambatana na vishindo vizito vya hawa watu ambao walikuwa ndani ya chumba hichi. “Ethan”

Niliisikia sauti ya Romani pembeni yangu.

“Mmmm”

“Upo sawa”

“Kidogo”

Romani akanifungua pingu nilizo fungwa, kisha akaninyanyua katika kiti hichi na kuanza kunisaidia kutembea.

“Ngoja kwanza”

Nilizungumza huku nikiangaza angaza humu ndani.

“Vipi mkuu”

“Nahitaji kuhakikisha yule mama aliye kuwa amenipatia mateso amekufa”

Romani akanivalisha miwani ambayo ina uwezo wa kuona kwenye giza totoro. Nikaanza kuangaza ndani ya chumba hichi na kukuta maiti mbili za wale vijana wake huku mwana mama huyo akiwa hayupo kabisa katika eneo hili.

“Mkuu tuondoke muda ni mdogo”

Romani aliendelea kunisisitiza huku akishika mkono wnagu. Tukaanza kutoka ndani humu huku mapambano na watu hawa yakizidi kusonga mbele. Tukafanikiwa kutoka nje ya jengo hili ambalo lipo katike eneo la kama jangwa na mwanga mkali wa mbalamwezi umeweza kunisaidia kuona vijana wanne alio ungana na Romani jinsi wanavyo zidi kurudisha mashambulizi kwa watu ambao waliniweka chini ya ulinzi. Tukaingia ndani ya gari mbili aina ya Auid Q7 na kuondoka eneo hili kwa mwendo wa kasi sana.

“Nashukuru sana kwa kuja”

“Usijali Ethan ndio jukumu letu.”

Romani alizungumza huku dereva akizidi kuendesha gari hili kwa mwendo wa kasi.

“Shiti wanakuja”

Dareva alizungumza huku akitazama katika kioo cha pembeni mwa gari hili. Romani akaniishamisha chini ya siti kisha akafungua kioo kidogo na kujitokeza pembeni na kuanza kumwaga mvua ya risasi kuelekea katika gari zinazo tuandama.

“Naomba bastola”

Nilimuambia Romani na kumfanya arudi ndani ya gari na kunitazama.

“Ethan hili tuachie sisi”

“Wewe nina omba nina uchungu sana na hawa watu”

Romani akanitazama kwa sekunde kadhaa kisha akachomoa bastola yake moja aliyo ichomeka katika paja la mguu wa kulia. Nikaikoki bastola hii na mimi nikatoa mkono mmoja ulio shika hii bastola na kuanza kushambulia gari zinazo tufwata. Mashambulizi yetu yakazaa matunda kwani kadri jinsi tunavyo zidi kwenda ndivyo jinsi tunavyo zidi kuzisababishia gari hizo ajali.

“Plan B”

Romani alizungumza kwa kupitia kinasa sauti alicho kivaa sikioni mwake na kusababisha dereva wa gari la mbele yetu kukunja kulia huku sisi tukielekea kushoto.

“Tunaelekea wapi?”

“Kuna helicopter tutaikuta mbeleni huku. Endapo tutafanikiwa kumaliza hili jangwa salama”

“Tupo jangwa gani?”

“Sahara. Hapa tulipo tupo Sudan”

“Ina maana wamenileta katika nchi ya Sudan?”

“Ndio”

“Ni kina nani kwani?”

“Tukifika nchini Tanzania tutakuambia”

“Sawa”

Dareva akazidi kuendesha gari hili kwa mwendo wa kasi hadi tukafanikiwa kulimaliza jangwa hili. Tukaingia katika msitu mdogo na kukuta helicopter kubwa. Tukashuka ndani ya gari na kuingia katika helicopter hiyo, hazikupita hata dakika tano, wezetu ambao tulitengena nao, wakafika katika eneo hili, wakayateketeza magari haya kwa moto kisha taratibu tukaanza kuondoka eneo hili.

“Tunaelekea wapi?”

“Tanzania ila kwa sasa inabidi tukae mafichoni ili tuweze kusoma hali ya hewa”

“Hali ya Tanzania kwa sasa ipo vipi?”

“Hali si shwari wananchi wana andama wanahitaji uweze kuachiwa huru. Serikali kwa sasa haijatoa tamko lolote juu ya kuchukuliwa kwako na hapa ninavyo kueleza wananchi wamajikusanya katika ofisi za mkuu wa mkowa akihitaji uweze kuachiwa huru”

“Kwa nini serikali haijatoa tamko?”

“Hatutajua, ila hapa inaonekana kuna mipango mibaya ya chini chini ambayo ilikuwa ina endelea dhidi yako. Kuna hizi video tape zilizo kuwa zina rekodi matukio yote katika jengo hilo. Hivyo tunaweza kuistaki serikali kwa kila jambo baya lililo weza kutokea”

“Unataka kuniambia serikali ndio imehusika moja kwa moja kwa mimi kuchukuliwa na watu wale?”

“Ndio ni asilimia mia moja serikali ime husika. Ila kama huto jali tunaweza kuipindua hii serikali iliyopo madarakani hivi sasa”

Maneno ya Romani yakanistua sana kwani jambo la kuipindua serikali ni jambo jengine sana ambalo kichwani mwangu sikuweza kulifikiria kabisa.



ENDELEA

“Kupindua serikali hilo ni jambo jengine. Hii ni my person war sio ya taifa. Nitadili na kila mmoja ambaye hakika anajaribu kuingia kwenye zone yangu”

Nilizungumza kwa msisitizo na kumfanya Romani kutingisha kichwa kukubaliana na hili nililo lizungumza. Tukafika nchini Tanzania majira ya saa kumi na mbili asubuhi. Tukatua kwenye moja ya kiwanja ambacho kipo katika pori ambalo kwa haraka haraka sikuweza kulifahamu. Tukapokelewa na Qeen, Latifa pamoja na Claudia. Tukaingia katika magari matatu tuliyo wakuta nayo na kuondoka eneo hili.

“I miss you my love”

Latifa alizungumza huku akinifunika na koti kubwa kwani toka nilipo kumbolewa nikiwa na boksa yangu sikuweza kupata nguo ya kunifunika.

“Nashukuru”

Tukafika katika nyumba noja ya gorofa iliyopo katikati yam situ huu. Tukashuka kwenye magari haya na kuingia ndani ya hii nyumba ambayo ndnai ina kila kitu cha muhimu kuwemo ndani ya nyumba.

“Hapa ni wapi?”

“Tupo Bukoba katika msitu mmoja unaitwa Rubare”

Romani alinijubu huku akinitazama usoni mwangu.

“Ni eneo salama?”

“Ndio alina shida, tupo salama kabisa?”

“Sio hifadhi ya Taifa hili eneo?”

“Ni hifathi ya Taifa ila kuna wakuu nimeweza kuzungumza nao na hakuna ataweza kutusumbua. Nyuma ina system kamera zaidi ya mia nane na zinaonyesha karibia eneo lililo zunguka nyumba hii kwa kilomita zaidi ya tano. Hivvyo hata mtu akihitaji kuingia katika eneo hili tumaweza kumuona. Tumezungukwa na mito pamoja na wanyama wengi.

Maelezo ya Romani yakaendana kabisa na vithibitisho alivyo anza kunionyesha ikiwemo mfumo mzima wa kamera hizo zilizo fungwa katika eneo hili.

“Kabla siku haijapita nahitaji kumjua yule mama aliye nipatia mateso”

“Sawa Ethan”

Tukaongozana na Latifa hadik katika chumba chetu. Moja kwa moja nikapitiliza hadi bafuni na kuanza kuusafisha mwili wangu ambao una maumivu kila sehemu.

“Nenda kanitafutie dawa au sindano ya kupunguza maumivu mwilini”

“Sawa mume wangu”

Latifa akatoka ndani humu na baada ya muda kidogoa karudi na vidonge viwili.

“Romani amesema vidonge hivi vitatuliza maumvi na vitakupatia usingizi mzuri kidogo”

Latifa akanikabidhi vidonge hivi viwili na nikavimeza.

“Jamani hata maji”

“Niletee”

“Sasa umesha meza mume wangu maji ya nini tena”

Nikamaliza kuoga na kurudi chumbani, nikajitupa kitandani huku kichwa changu kikiendelea kumfikiria mwana mama yule ambaye amenipatia mateso ambayo kwenye maisha yangu sikuwahi kuyafikiria siku hata moja kama ninaweza kukutana nayo. Usingizi taratibu ukaanza kunichukua na mwisho nikajikuta nikilala usingizi fofofo.

***

Baada ya siku tatu hali yangu ya ikaanza kurudi katika hali yake ya kawaida huku maumivu yakipungua kwa kiasi kikubwa.

“Huyu mama familia yake ipo Arusha. Ana watoto wawili, mmoja ni wa kiume ana jitegemea kimaisha ni mfanya biashara na huyu wa kike yupo chuo ana somea maswala ya uandishi wa habari”

Romani alizungumza huku akinionyesha faili lenye taarifa za mwana mama huyo aitwaye Lucy Kavishe.

“Mwana mama huyu pia ni usalama wa taifa na ana miaka thelathini na sita sasa kwenye kazi yake hiyo”

“Okay yeye kama yeye tutampatia wapi?”

“Hadi sasa hivi tumechunguza ila hatujajua ni wapi tunaweza kumpata.”

“Basi nahitaji huyo mwanaye wa kiume muweze kumuweka mikononi”

“Si wa kike?”

“Wa mama wengi wanapenda sana watoto wao wa kiume na wengi wao wanaficha siri za watoto wao wa kiume. Hivyo hakikisha kwamba tuna tuna muweka kizuizini huyo kijana”

“Sawa Ethan”

“Pia hakikisheni kwamba muna fwatilia nyendo za Biyanka”

“Nimekuelewa”

Romani akaondoka na vijana wake ambao alinieleza kwamba ni watu alio wahi kufanya nao kazi katika mataifa mbalimbali nje ya Tanzania na wapo vizuri katika maswala ya ujasusi.

“Unataka kumfanya nini huyo kijana?”

Latifa aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.

“Nahitaji kumtumia yeye kumpata mama yake”

“Huoni kama inaweza kusababisha matatizo zaidi mume wangu”

“Hadi sasa hivi tuna matatizo. Kitu ambacho nina hitaji kukifahamu kwa yule mwana mama ni kwa nini alikuwa ana nipa adhabu ambayo kwa haraka haraka ilikuwa ni kali sana na haivumiliki”

“Kama ulivyo niadiasia labda waliona ndio njia sahihi ya wewe kusema”

“Sawa ila kuna vitu dhairi ana onekana alikuwa akivifanya kwa ajili ya chuki”

“Wewe na yeye muna fahamiana?”

“Hapana ila nakumbuka kuna kauli moja aliizungumza tukiwa ndani ya gari. Aliniambia kwamba Biyanka sijui ata niua kwa mkono wake mwenyewe. Sasa hapo ndipo ninapo jikuta nikihisi kwamba japo yupo ndani ya serikali na alinikamata kutokana na sheria inavyo mruhusu kunikamata ila naamini ana tumikishwa na Biyanka”

“Ndio maana nilikuwa ninakuambia tusimuache aondoke yule mwanamke. Kwa maana kama yeye na baba yake ni kitu kimoja na baba yake ame fariki dunia basi kwa asilimia mia moja ni lazima ata amini kwamba wewe ndio muuaji wa baba yake na lengo lake nahisi alihitaji kupata udhibitisho kwamba wewe ndio umemuaa baba yake na angejua nini cha kufanya”

“Hembu mpigie simu Romani”

Latifa akafanya hivyo kisha akanikabidhi simu hiyo.

“Romani”

“Ndio mkuu”

“Zile tepu za yale matukio ambayo nilikuwa nina fanyiwa kule nilipo kuwa nime tekwa unazo?”

“Ndio ninazo na video hizo nimesha ziweka kwenye flash mbili moja ninayo na nyingine muambie Claudia akupatie”

“Sawa”

Nikakata simu na kuelekea chumbani kwa Claudi amabaye kwa sasa tuna heshimia kama mtu na dada yake japo hapo awali tulijikuta tukiwa katika mapenzi mazito, ila kutokana moyo wake ume mchagua Romani sikuona haja wala sababu ya msingi kwa mimi kulazimisha penzi lake.

“Ethan karibu”

Claudia alizungumza huku akijifunga taulo vizuri mwilini mwake kwani nimemkuta akiwa ana toka bafuni kuoga.

“Asante kuna flash moja hivi Romani ameniambia unipatie”

“Ahaa ngoja nikutafutie”

Claudia akafungua droo ya dreasing table na kunikabidhi flash hiyo. Akanipatia na laptop ya mume wake kisha nikarudi sebleni.

“Jamani lunch ipo tayari”

Qeen alizungumza huku akiwa ame vaa nguo maalumu za kupikia jikoni.

“Sawa best”

“Ethan”

“Naam”

“Hembu njoo mara moja”

Nikaingia jikoni na kumkuta Qeen akifuta futa meza za jiko hili kubwa lenye makabati.

“Kuna juisi ya parachichi hapa nimekupatia. Hembu ionje kidogo kama ni nzuri”

Qeen alizungumza huku akinimiminia juisi hiyo kwenye glasi ndogo hivi. Nikaionka taratibua.

“Mmm ni tamu sana”

“Kweli?”

“Yaa nimeipenda. Hii hii ni nzui”

“Basi ombi langu lilikuwa ni hilo”

Nikaelekea sebleni na kumkuta Latifa akiwa ana nisubiria. Nikaichomeka flash kwenye laptop hii na kuanza kuangalia jinsi nilivyo kuwa nikiteswa kwa mateso makakali sana. Latifa hakuweza kumalizia video hii na kujikuta akiifunika laptop hii.

“Inatosha Ethan”

“Inatosha nini?”

“Ethan unahisi kwamba nina ujasiri wa kukutazama jinsi ulivyo kuwa unateseka hapo. Sina roho hiyo, yaani nikiona chozi lako kwangu nina hisi kama moyo wangu una kwenda kuvunjika na kung’oka.”

Latifa alilalama.

“Mwanamke mbona una lalama”

Qeen alizungumza huku akiweka chakula alicho pika katika meza ya chakula.

“Kuna video ya mateso niliyo kuwa nina teswa eti ameshindwa kuitazama”

“Hembu nione”

Qeen akaichukua laptop hii na kuanza kuitazama video hii. Hadi ana maliza kuitazama uso wake wote umejawa na machozi mengi sana.

“Kumbe ndio maana una msaka sana huyu mama?”

“Ndio”

“Haki ya Mungu huyu Ethan endapo una mshikilia mikoni mwako. Hakikisha kwamba humuachi hai”

“Akileta sababu ya mimi kumuua basi nitamuua, ila akileta sababu ya mimi kumuacha hai basi nitamuacha hai”

“Hana sababu ya kukufanya umuache hai. Ethan unatakiwa kufanya jambo katika hili”

“Nahitaji kuiweka hii video kipande kidogo cha sekunde kumi na tano kwenye akaunti yangu ya Instergram”

“Mmmmm”

“Ndio nahitaji kuiweka na hitaji kuionyesha ulimwenguni kwamba hii ndio hali ambayo nilipitia”

“Muda wake bado mume wangu. Dunia kwa sasa hawajui ni wapi ulipo, ila hembu kuwa mvumilivu katika hilo”

“Hata mimi nina muunga mkono Latifa hakuna haja ya kuiweka hiyo video kwenye mtandao. Hembu tumalize jambo la kumsaka huyo mwana mama”

“Nimewaelewa”

Taarifa ya habari inayo endelea kwenye televishion hii ikatustua mara baada ya raisi aliye shinda uchaguzi ambao ulifanyika mwenzi uliopita kupata mstuko wa moyo na hivi sasa hali yake ipo vibaya.

“Hapa kuna kitu kinacho endelea”

Nilizungumza huku tukitazama helicopter ya raisi ikiwa imetua katika kiwanja cha hospitali kuu ya taifa ya Muhimbili.

“Ila kama alikuwa na matatizo ya moyo hilo ni jambo la kawaida tu”

“Hapana sina hisia kwamba ni ugonjwa. Mtu asimame majukwaani kwa kipindi cha mwenzi mzima alafu leo hii uniambie kwamba ame pata mstuko wa moyo”

‘Amewekewa sumu’

Nikaisikia sauti ya Ethan masikioni mwangu na kujikuta nikistuka sana. Nikaondoka sebleni hapa na kuingia chumbani kwangu na kufunga mlango.

“Ulikuwa wapi siku zote nilizo kula msoto”

Nilimuuliza Ethan aliye simama kwenye kioo cha dreasing table iliyopo ndani hapa.

“Vita haijakwisha bado”

“Una maana gani?”

“Una kumbuka black box?”

“Ndio”

“Hilo ndio jambo linalo endelea hivi sasa. Ile fumular ya utengenezaji wa bomu za nyuklia bado ina sakwa na watu hao macho yao yapo kwako hivyo bado hujamaliza vita”

Nikabaki nikiwa nimejawa na mshangao mkubwa sana kwa maana swala la Black box nilisha lisahau kwenye ufahamu wangu wa akili.

“Nani yupo nyuma ya hili?”

“Camila”

“Camila kwa nini?”

“Yeye ndio mtu wa pekee ambaye alikuwa ana lielewa hili jambo na kumbuka alihitaji kukuaa pia kutokana na jambo hilo. Hivyo kutokana kwa sasa hamuna mahusiano yoyote hivyo ana kusaka”

Nikashusha pumzi taratibu huku nikikumbuka mambomengi sana ya maisha ya nyuma ambayo kwa kipindi hicho nilikuwa bado ni kijana mdogo mno.

“Hili swala la kuchukuliwa na kuteswa nalo vipi?”

“Hapo ni Camila, wameungana na Biyanka. Maadui wamekuwa sasa ni kitu kimoja na wao ndio wanao kuwinda. Biyanka alihitaji ukiri ili hukumu itakayo toka hapo ni ya wewe kunyongwa. Ila kabla hujanyongwa basi Camila atahakikisha kwamba ana kubana mpaka una pata hiyo fumular ya kutengeneza bomu la nyuklia.”

Ethan alizungumza kwa msisitizo huku akinitazama usoni mwangu.

“Nakumbuka walisema fumular hiyo ipo kwenye mwili wangu na sehemu niliyo chanwa haikuonekana je ipo wapi?”

“Ndio bado ipo mwilini mwako”

“Sehemu gani?”

Ethan akaniomba nivue shati na nikafanya hivyo. Akanigusa mgongoni na mkono wake wa kulia na hapo ndipo nilipo anza kuona michoro ya tattoo ikianza kujitokeza mgongoni mwangu, ambayo katika kipindi chote cha maisha yangu sikuwahi kuiona wala mtu yoyote kuweza kuiona kwa macho ya kawaida.

“Hiyo ndio ramani ambayo itakupeleka moja kwa moja sehemu ilipo fichwa black boks “

Ethan alizungumza kwa sauti ya upole sana.

“Ipo nchi gani?”

“Ujerumani”

“Kwa hiyo una hitaji niweze kwenda nchini Ujerumani?”

“Ndio unatakiwa kuhakikisha kwamba una ungana na Piyanka na utekeleze lile swala zima la kuhakikisha kwamba una tengeneza visima vya kutengenezea silaha za nyuklia”

Nikashusha pumzi taratibu huku nikimtazama Ethan usoni mwake.

“Nahitaji kudili kwanza na yule mwana mama”

“Achana naye yule hana chochote cha kukusaidia”

“Kwa nini?”

“Fanya hicho nilicho kueleza. Wasiliana na Piyanka kisha muongozane kuelekea Ujerumani?”

“Mimi kurudi Ujerumani haito leta mashaka na wasiwasi kwa watu?”

“Hakuna jambo kama hilo. Wewe fanya hicho nilicho kuambia.”

“Biyanka na Camila nitapambana nao vipi?”

“Pata kwanza hiyo fomular kisha mambo mengine yatafwata”

Ethan akapotea kwenye uwepo wa macho yangu. Nikatoka sebleni, na kuichukua simu yangu na kurudi chumbani. Nikampigia simu Romani na kumuuliza juu ya oparesheni yao jinsi inavyo endelea.

“Hadi sasa tupo katika hatua za kumkamata kijana wa yule mama”

“Aihirisheni huo mpango?”

“Kwa nini mkuu?”

 ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

BLOG