Search This Blog

Saturday, February 26, 2022

SEKESEKE (ROHO MKONONI) - 5

   

Simulizi : Sekeseke (Roho Mkononi) 

Sehemu Ya Tano (5)


"Wote kimyaaa..."


Ghafla sauti kali tena ya amri ikasikika kutoka nje ya selo ile kubwa ya wa babe triple c,wengi waliijua sauti ile aikuwa ya mwingine zaidi ya ya mkuu wa gereza lile Gerald Dunga.


"Umefanya kosa sana kumpiga nyapara wako ni kama umenipiga mimi,sasa hukumu yako ni hapa hapa iwe fundisho kwa wengine"


Dunga aliongea kwa ukali akachomoa bastola yake ndogo na kumuelekezea Butu,akipanga amtandike na kumuulia palepale kama alivyoambiwa na mkurugenzi wa usalama wa taifa mr Zidu kite.akaikoki bastola tayari kuiruhusu kuchomoka,Butu alibaki katika bumbuwazi kutokuamini kile kinachotokea,kupata adhabu ya kifo kisa kosa la kupigana?!,hakika jambo hili lilimshangaza sana...


Sasa kidole cha pili baada ya dole gumba cha Dunga,kikawa kinaenda kushika kinasulio,kuruhusu risasi kuchomoka.


Majanga!.



Sekeseke la hatari bado lina ya andama Maisha ya alokuwa Inspekta wa jeshi la polisi John Butu, baada ya kusalimika ndani ya lango la jehannamu anapelekwa katika selo ijulikanayo kwa jina la trple c,huko anakutana na nyapala Manzua,nyapala alopewa kazi ya kumtesa Butu ikiwezekana kumuua kabisa,kazi inakuwa ngumu kwa Manzu hatimaye anapigwa yeye,kitendo cha kupigwa kinawafurahisha wafungwa na hata maaskari pia kwani wengi walimchukia Nyapara yule,je nini kitaendelea?!,tusonge katika hatua inayofuata...


HATUA YA ISHIRINI NA NNE


Kabla Mkuu wa Magereza Dunga ajaruhusu risasi kutoka katika bastola yake,ghafla ikasikika sauti nyuma.


"Hapana mkuu usifanye ivyo!.."


Ikabidi mkuu yule wa gereza ageuke nyuma,macho yake yakatua kwa kijana mdogo alokuwa ndani ya sare nadhifu za jeshi la magereza,mabegani kwake akiwa na nyota mbili akipishana naye kwa nyota moja tu yeye alikuwa na cheo cha kapteni akimiliki nyota tatu.


Usoni mwa kijana yule alipambwa na tabasamu jepesi,akamfikia Kapteni Dunga bado tabasamu likipamba mdomo wake.


"Unataka kuniambia nini Luteni?!"


Dunga akaongea kishari mkono wake wenye silaha ukiwa una angalia chini,kijana yule alojulikana kwa jina la Luteni Johnson Mamba ndo alikuwa msaidizi wake,alimfikia akamshika mkono na kumkokota mpaka nje.


"Mkuu punguza hasira kumbuka huyo ni mwanausalama tena inspekta wa polisi je unadhani ukimtandika risasi jeshi lita acha kufatilia na mashahidi niwafungwa utakaa pabaya mkuu"


Wakati wakielekea ofisini Johnson akatumia wasaha huo kumshauri mkuu wake,hata Dunga alipofikiria ni kweli,jeshi la polisi lazima lingechunguza kijana wake kafa katika mazingira gani!,na ingejulikana kuwa yeye ndo kamtandika risasi tena hadharani angejiweka pabaya!.


"Lakini ilikuwa ni oda ya usalama wa taifa!,"


Dunga akaongea kwa sauti ndogo,sauti ilojaa wasiwasi tele!,


"Hata kama mkuu ni oda ya usalama wa taifa ndo si umuue hadharani,lazima upange mpango kabambe ikiwemo kuamishwa gereza then njiani gari ivamiwe auwawe,au njia nyingine yeyote ambacho kifo chake akitokuwa cha utata!"


Wazo lile dunga moja kwa moja akakubaliana nalo,alipofika ofisini kwake akaongea na Zidu juu ya mpango aloupanga kwamba ata andika barua kwa general kuomba kuamisha wafungwa kadhaa sababu ikiwa wingi wa watu,siku ambayo hata amisha wafungwa atamjulisha aandae vijana wake wavamie msafara na wajifanye kumtorosha Butu hapo askari wake wamuue kwa kumtandika risasi,hii isingeleta shida wala upelelezi ndani ya jeshi la polisi.

Pasina kupoteza muda Kapteni Dunga akaandika barua kwa General,ambapo baada ya kuituma siku ilofatia,kesho yake akapokea majibu kwamba Gereza la keko lishajulishwa hivyo aandaye hao wafungwa katika karandinga wasafirishe...


***


Kwa upande wa Butu maswali mengi bado yaliushambulia ubongo wake hasa tukio la mkuu wa magereza kumnyooshea silaha.


'ina maana kama si kutokea Jonson,Dunga angemtandika risasi na kumuulia mbali?!,kisa tu kampiga nyapara?!'


Jambo hilo alilifikiria sana alikumwingia akilini!,alijua lazima kuna kitu kinachoendelea dhidi yake!,akakumbuka yani yeye kuja tu,pasina kosa lolote akaswekwa lango la jehannamu tena ndani ya masaa 24 sawa na siku mbili za kifungwa,lango la jehannamu mahali wawekwao magaidi,majambazi sugu makatili,na viumbe visivyo stahili kuishi!,iweje awekwe yeye?!,yeye aloitumikia serikali tena idara ya polisi ulinzi na usalama wa raia na mali zake leo wamlipe vile?!,yeye ilipaswa awekwe triple A,iweje awekwe triple c?!,kwa uzoefu wake wa kipolisi akamtilia shaka mkuu wa magereza,akajua lazima anatumika,na maisha yake si salama,akajua ilipaswa afanye kitu haraka,kukaa pale ni sawa na kukisubiria kifo,na kingemkuta!.


Sasa angetokaje hali ya kuwa hata kazi nje akuruhusiwa kwenda kufanya pengine angefikiria kutorokea huko.


Japo kwa sasa Gereza lilimuheshimu hakukuwa na alothubutu kumtishia si nyapara,wala magwa,katu akujua hatari aloandaliwa...


Siku ilofatia asbuh alishangaa akiitwa akaelekea mpaka kwa mkuu wa magereza ndani alikuta pia wafungwa wa kutosha,huko ndipo walipoambiwa wa na amishwa gereza,hivyo wakatolewa chini ya ulinzi mkali,wakapakiwa katika karandinga lililozungushiwa nondo ndogondogo kwenye bodi,safari ikafatia wakisindikizwa na gari mbili za polisi


Tayari Zidu alisha waandaa vijana wake wa kutosha eneo la tukio tayari kwa uvamizi pale gari la magereza litakapowafikia.


Butu akujua hili wala lile,safari ikaendelea!....




Gari ilobeba wafungwa ilizidi kukata mbuga huku mbele yake pakiwa na kitara cha polisi na nyuma ikiwepo cruzar ya polisi ikiwa na maaskari takribani wa tano wenye mitutu waloivaa vifuani mwao,kitara cha polisi kilikuwa na askari wa tatu tu pale mbele,safari iliendelea na sasa walikuwa wakiikaribia keko,ila wakiwa katika eneo moja nyuma kidogo ya daraja Swami kitara cha polisi kilisimama,mbele yake paliwekwa mawe makubwa,dizaini kama kuzuia njia,


Askar wale wawili wakashuka kwa lengo la kwenda kutoa yale mawe yaliyopangwa chiani!.


Kosa!.


Ng'afla milio ya risasi ikasikika punde watu wasopungua kumi waloficha nyuso zao wakatokea toka chini ya daraja na kuanza kuwashambulia wale maaskari,wale walokuwa nyuma kuona hivyo nao wakashuka na kuwatupia risasi wavamizi,ila askari walizidiwa na mwisho kusamli amri,wavamizi wale wakaomba wapewe Butu gari ikafunguliwa Butu akatolewa,kisha maaskari wakaruhusiwa kuendelea na safari.


Kitendo kile kiliwashangaza sana wale wafungwa,askari kusamli amri,kukubali kuachia mfungwa pasina kupata jeraha hata moja,kila mmoja alisema lake,ila safari iliendelea.


Hawakuwa na uhuru ni wapi wangepeleka wasiwasi wao?!.


Kwa upande wa Butu machale mapema yalishamcheza hasa baada ya kuona urushianaji wa risasi kati ya pande mbili zile,ulikuwa ni wa uangalifu kuto mlenga mwenzake,kichwani mwake akajenga picha kuna kitu kinachoendelea pale,alikamilisha wazo lake baada ya kuona maaskari eti wanasamli amri na mwisho kukubali kumtoa nao kuendelea na safari yao.


Kipo wapi kiapo walichokula?, kupambana kufa kupona kulinda raia na mali yake,kivipi wakubali kumtoa kwa watu wasojulikana?!,alijiuliza pia je wale ni watu wa aina gani waloamua kumsaidia?!,alijua kwa kipindi kile hapakuwa na msaada wowote kwake asitegemee.


Watu wale walimswaga mpaka mahali walipoifadhi magari yao,walikuwa na magari matano,wakamwingiza katika gari moja wapo wengine wakaingia katika magari yao,yeye bado alibaki na butwaa akitafakari wale ni watu gani na li lipi lengo la wao kumchukua?!...


"Unapaswa ufungwe macho upaswi kujua ni wapi unapelekwa,kingine kaa utulie atutakufunga miguu wala mikono ila tuki gundua unataka ulete janja ujanja fulani hatutosita kukumaliza hata kabla ya muda tulokupangia kukuua nadhani tume elewana?!".


Mtu mmoja alimuongelesha Butu hata hivo kijana yule akujibu kitu,mtu yule akampa ishara mwenzake amfunge macho Butu kusudi asijue anapopelekwa,naye akatii hilo safari ikaendelea.


Redio ikawashwa njia nzima watu wale wakawa wakizungumzia maswala ya wasanii,Butu hakazidi kushangaa kwani alijua labda hata angepata chochote katika maongezi yao,alikaa kwenye gari mpaka akachoka,akujua ni wapi anapelekwa njiani ni kama alitembea masaa matatu hatimaye gari ilisimama.


Akajua sasa kashafika,akashushwa akakokotwa pasina kujua ni wapi anapelekwa ila aliweza kung'amua kuwa yupo msituni kwani alizisikia sauti za wanyama,na hata ndege pia aliundua kuna muda alikanyaga majani kuna muda alipishana na miti mwisho akasikia mmoja akisema...


"Dula hapa panatosha!"


Palepale akabwagwa chini akafunguliwa kitambaa sasa alipata kuona vizuri mazingira ya pale alipokuwepo.


Ni katikati ya msitu,tena katikati ya vichaka mbele yake akizungukwa na wale watu kumi tena wakiwa na silaha.


"Una dakika tano za kuvuta pumzi ilobakia,ndani ya dakika hizo waweza zitumia,'a' kwa kusali Allah aipokee roho yako na kuitunza mahali pema peponi amin,'b'kujitetea ama kwa kupambana na sisi au tukuruhusu ukimbie na che tunakupa nafasi uliza chochote,swali moja tu!,tutakujibu.


Butu alijua sasa anaenda kufa lakini huzuni yake kubwa anakufa bila kumlipizia aloiteketeza familia yake,anakufa na kinyongo,akajikuta machozi yakimchuruzika,ila

akakumbuka ana dakika tano tu alizopaswa achague,alitamani amjue mbaya wake,ila akuona uhafadhali huo hali ya kuwa anaenda kufa akaona ni bora tu asali sala zake za mwisho roho yake ipokelewe,baada ya dakika zile kuisha ndipo silaha zilipo mwelekea ni kwamba angetandikwa zote kumi kwa mara moja uwezekano wa kuendelea kuishi kwake usingekwepo.


"Kabla atujakuua nimeona ni vyema pia kukupa nafasi ya upendeleo uzitambue sura zetu sisi wauwaji wako!"


Palepale watu wale waka anza kuvua sox zile walizovaa vichwani.


Butu kuwaona tu watano kati ya kumi wale aliwatambua.


vipara.


Ndiyo ni wale waloshuka kwenye ndege siku ile wakiwa na madawa ya kulevya akawakamata na kuwatia ndani,simanzi ikamtawala upya,mabwana wale vipara,walimtazama kwa matabasamu mabaya,yalojaa dharau,kisha wakapeana ishara palepale milio ya risasi ikasikika.


Risasi kumi zikikishambulia kifua cha Butu akaporomoka chini,na kutulia tuli,mmoja wa watu wale akaenda na kusikiliza mapigo ya moyo yalitulia,akageuka na kumwonesha mwenzake ishara ya dole,mmoja mwenye kamera akaupiga mwili ule picha kadhaa.


"Mkuu tushaikamilisha kazi vipi huu mwili tuache huku?!".


"No! hiyo ni mali ubebeni muulete hapa kwangu haraka kesho usafirishie mzigo"


Palepale mwili wa Butu ukabebwa na kuwekwa nyuma ya buti kwenye tax moja wapo kati ya zile gari,safari ya kurudi mjini ikafatia...





John Butu anatandikwa risasi kumi na kupoteza fahamu,watu wale wakijua wamesha muua wanambeba na kumuingiza ndani ya Buti ya gari yao,je unadhani nini kiliendelea?!...


Tusonge katika hatua inayofatia


Baada ya kuuingiza ule mwili ndani ya Buti safari ikafatia.


Mwisho wa safari ulikuwa ni katika jumba la kifahari la Zidu,jumba ambalo ulitumia kufanya mambo yake ya siri,mwili ule ukatolewa na kuingizwa katika chumba maalumu,vijana wale wa usalama wa taifa hatimaye wakaondoka.


MASAA MATATU BAADAYE


Walinzi walifungua lango gari kadhaa zikaingia,zilielekea mpaka maeneo ya maegesho zikapakiwa vizuri kisha walokuwa ndani ya magari yale wakashuka,wa kwanza akiwa Zidu mwenyewe akaenda kufungua mlango,vijana wale waloshuka walielekea nyuma ya buti zao walipofungua na kutoa miili ya watu wakaingiza ndani,kule alipowekwa Butu,baada ya kukamilisha kazi yao wakarudi katika gari zao wakaingia na kutoka.


Zidu alielekea mpaka sebuleni kwake akaketi kochini,sasa alihitaji kumjulisha mh Rais walipofikia,akashika simu yake na kutafuta namba alizohitaji alipozipata akazitwanga,zilihita hatimaye zikapokelewa...


"Mh Raisi nimefanikiwa kuileta ile miili mpaka hapa pardon je kipi kifatie?!"


"Vizuri sana,ngoja niongee na dk Stanley aje aipasue hiyo miili na kuiyewekea mizigo mara moja kesho asubuh isafirishwe,then itapaswa iondoke na wamama wa tano ambapo watarudi nayo ikiwa na mizigo mingine sawa?!"


"Sawa mkuu!"


Kweli baada ya nusu saa gari ya dokta ikawasili,akiwa na msaidizi wake,dokta alikuwa kakunja sura akuipenda ile kazi sasa angefanyaje na ni amri ya kiongozi wa nchi,haraka wakaingia katika chumba kile cha siri,waka anza kuifanyia operesheni miili ile mitano na kuiweka kiasi kikubwa cha madawa katika matumbo yao,dokta alishtuka baada ya kuukuta ule mwili wa mwisho ukiwa na uhai,japo mapigo yake yalipiga kwa mbali!.


Akajikuta moyo ukimsuta,wajibu wa kazi yake ukamvaa,dhima ya kazi yake ni kupigania maisha ya kiumbe kilicho mahututi kuhakikisha kinakuwa hai,hapo ndipo ilipofuraha ya daktari yeyote ulimwenguni,akampa ishara msaidizi wake,operesheni ikaanza,kwanza kwa kumtolea risasi zote kumi,mwisho maswala ya kitabibu yakafatia,masaa manne wakaitimisha operesheni ile,sasa Butu alilala kitandani akitumia mashine za oxygen hali yake bado ilikuwa mbaya.


Masaa yakakatika hatimaye Zidu akawasili toka kazini alipoelekea ile mida ya mchana,baada ya kuwasili kwa daktari.


"Vipi kazi imekamilika?!"


Zidu akamuhoji daktari yule huku akiketi sofani.


"Ndiyo mkuu ile miili mitano mfu nimeipandikiza viroba vya unga ulivyo nipatia ila ule mwili mmoja nimeukuta una uhai nimeufanyia operesheni japo hali yake bado mbaya kupona ni kudra za Mungu..."


Zidu akakunja sura,hasira zikampanda.


"Kwani uliambiwa uje utibu hapa au upasue matumbo utie unga ndani yake na kuyashona?!"


"Lakini tahaluma yangu ainitumi kufanya hivyo kwa kiumbe hai!"


Dk Stanley naye akaja juu,.


"Kwa hiyo pakiti moja ujaliweka ndani ya tumbo la mtu?!"


"Yah nimefata maelekezo kama ulivyo nambia kila mwili nitie kiroba kimoja na ndivyo nilivyofanya,kasoro tu kwa huyo kiumbe hai,nimemtoa risasi nikamfanyia opereshen now nimemtundikia dripu na anasaidiwa na mashine za kupumulia".


"Aaah!,comon dk unafanya nini?,ujui yule mtu ana hatari gani kwa taifa ingali akiwa hai,yapaswa ukamuue mara moja na utie hayo madawa katika tumbo lake muda wowote mheshimiwa anawasili sijui tutamjibu nini!?"


"Hapana mkuu utanisamehe bure kazi yangu mimi ainitumi kuua,kwa hilo sitokuwa tayari!".


Daktari akazidi kubishana na Zidu pasina kujua yule ni kiumbe katili kwa kiasi gani,mapigo ya moyo yakazidi kumwenda kasi akazidi kujiuliza yule dokta ni wa aina gani mpaka awe na ujasiri wa kubishana naye?!,kipi kinacho mfanya ajiamini kwa namna ile?,akajikuta akiwaza sasa kutumia nguvu kuiendesha ile kazi hata ikibidi kuua aue kama ato muelewa!,.


"Dokta kama unayapenda maisha yako,naomba fanya kazi nilokuagiza taratibu geuka twende chumbani ukaue yule kiumbe umwekee hiyo pakiti ilobakia hapana muda tena wa kupoteza."


Tofauti na mategemeo yake dk aka achia tabasamu tena lile la madharau,kisha kwa sauti ndogo ila ya kujiamini akageuka...


"Unantisha siyo?,unadhani nina nidhamu ya uoga siyo?!,tandika risasi uzitakazo lakini siwezi badilisha ukweli,siwezi ua kiumbe kilicho hai nilichopoteza muda wangu kukitibu,jasho limenitoka pale labda uue wewe lakini mimi akaa utansamehe tu bure."


Kuongea vile akawa kampa wazo Zidu,kuliko kubishana na kupoteza muda mbona yeye ana weza kwenda na kumuua kwa sekunde chache kwa kumtandika risasi nyingine zisizo na idadi?!


Kwa haraka akageuka na kuelekea chumbani,dokta akimfata nyuma alipofika akafungua mlango bastola mkononi akaielekezea kitandani pale alipo Butu,alijua labda dokta angemzuia ila dokta alibaki tu kumwangalia,taratibu akapeleka kidole chake katika kifyatulio kwa lengo la kuruhusu risasi ichomoke safari hii kwa hali alokuwa nayo Butu sijui kama angepona!..


Sijui kwa kweli.......





Butu anachukuliwa kwa lengo mwili wake ukatumike kubebea na kusafirishia madawa ya kulevya nchi za nje ikiungana na mihili mingine kumi.


Kwa bahati nzuri Dokta ajulikanaye kwa jina la Dokta Stanley anagundua Butu yu mzima haraka sana anamfanyia operesheni ya kumtoa risasi zote kumi kitendo hiki kinazua Sekeseke jipya kwa Zidu,


Anamjia juu daktari.


Maisha ya Inspekta Butu yanakuwa Roho mkononi,mabishano makali yanaendelea mwishoni Zidu mwenyewe ana amua kuzama ndani ya chumba kile akamalize kazi mwenyewe bastola mkononi anaielekeza pale alipo Butu je atammaliza?!....


Ungana nami katika hatua inayofatia kuzidi kuburudika zaidi


HATUA YA ISHIRINI NA SABA.


Kabla ajamtwanga ile Risasi ghafla akasikia sauti nyuma yake.


"Zidu achaaaaa...."


Kisha hatua tena zikipigwa haraka haraka kuja ule upande wao.


Sauti ile aliijua fika,ilikuwa ni ya mheshimiwa Rais,mapigo ya moyo yakaanza kupiga kwa kasi si yeye tu lah hata kwa daktar Stanley naye alitetemeka binafsi aliutambua ukatili wa Raisi wake yule akajua hapo pangenuka tu na si kwake hata kwa Zidu pia ila hata ivyo akujali.


Moyo wake ulisimama katika haki,alikuwa tayari kufa ila si kuua kiumbe kisicho na hatia hiyo kuziwekea tu zile mwili viroba vya madawa moyo wake ulikuwa ukimchuruzika machozi kwa uchungu sembuse kuua?!.


Hapana hakuwa tayari kwa ilo.


Itakavyokuwa na iwe,akawa tayari kupokea lolote lijalo.


Raisi Patrick Bisau akawafikia pale walipo.


" Zidu amna haja ya kumuua huyo kwani inatakiwa miili Kama hii mitano kwa ajili ya kusafirisha mizigo USA hivyo dokta katufanyie mchakato ya miili minne katika hospitali yako dokta Julias atafanya hiyo kazi ya kuiwekea mzigo sawa?!,Zidu hii itangulie uwanja wa ndege kwa Safari ya kuelekea hapo kenya wale wa mama wa msiba si ushaongea nao?!..."


"Ndio mkuu nishawapanga watakuwepo KEIA kuipokea miili Kama ya ndugu zao"


"Very nice kazi nzuri mpigie Isack,Kinampa waje mkaipakie hii miili DIA haraka sana na Isack asafiri nayo wewe utaelekea USA na hii miili mahututi na madokta hawa sawa?!"


"Sawa mkuu"


Zidu akaitika,palepale Raisi aka aga na kuondoka,mzigo wote ulikuwa katika jumba lile la Zidu na kazi ilifanyikia pia palepale.


Baada ya muheshimiwa Bisau kuondoka Zidu na dokta wakatazamana hakuna alotoa neno kwa mwenzake kila mtu akaendea na shughuli yake.


Dokta Silvestar akaelekea mpaka mahali alipo msaidizi wake akampa maelekezo.


"Doto mimi natoka hakikisha usalama wa mgonjwa wangu mpaka hapo dokta Julias atakapowasili badiliko lolote litakalotokea utanijulisha sawa?!"


"Sawa dokta"


Binti yule nesi akaitikia kwa heshima,daktari akatoka zake,tayari kwa kwenda kutekeleza jukumu jipya alilopewa na mkuu wake.


Zidu mapema sana yeye alishaondoka yeye hakuwa na wa kumpa maelekezo pale.


***


*SURA YA SITA*


*UNITED STATES OF AMERICA*


*WASHINGTON DC*


Ndani ya taifa la marekani katika mji mkuu katikati ya jiji katika jengo moja kubwa lenye ghorofa zaidi ya 30 jengo hilo kubwa lilimilikiwa na bilionea alotambulika kwa jina la Mernly Max Arthur.


Ndani ya chumba kimoja juu kabisa ya ghorofa kulikuwa na kikao cha siri ni baada ya taharifa nyeti kutua kwa bilionea huyu Merly kwamba kuna kiasi kikubwa Cha madawa ya kulevya kinaingia nchini kwa njia ya magendo kutoka nchini Tanzania akakumbuka miaka mingi nyuma alishawai kutapeliwa na huyo mwenye mzigo huo kipindi hiko Bisau akiwa mgombea pesa hizo akazitumia kuimarisha chama na kuendeshea kampeni.


Kwa muda mrefu sasa Merly amekuwa akimfatilia Raisi Bisau kwa kusudi la kulipiza kisasi bila mafanikio ila mtafutaji huwa akosi siku hiyo hatimaye habari zikamfikia kuwa watu mzigo unaingizwa na wagonjwa mahututi haraka akaweka kikao kujadili swala Lile.


Alikuwa kavimba kwa hasira,


"Niliapa siku moja kulipiza kisasi kwa kile Bisau alichonitendea na muda ni Sasa sitokuwa na msamaha kwa hili!,alinirudisha nyuma sana Sasa Agent Bray hakikisha unakusanya vijana wako wakakamavu mnawasili uwanjani na ambulance mnawapokea hao wagonjwa Mimi nishawapanga Madison's Hospital ndo walikuwa wawapokee watachelewa kwa dakika tatu nanyi mtazitendea haki kumbuka ni dakika tatu tu..


Agent Bray nakuamini nimekusomesha na Sasa ni mpelelezi unaye tegemewa, na taifa letu la Marekani usije ukaniangusha kwa hili nitampiga huyu fala pigo ambalo hatokaa alisahau katika maisha yake na huu ni mwanzo naapa one day nitahakikisha anakufa na Tanzania inatawaliwa na kiongozi safi Raisi gani anauza madawa ya kulevya?!"


Max Merly aliongea kwa uchungu.


Agent Bray alitabasamu akamtoa khofu mkuu wake kwamba kazi ataifanya Vizuri.


Kwa upande wa Tanzania miili ile mitano ilipasuliwa ikatiwa madawa siku ilofatia ikapakiwa kwenye ndege binafsi Safari ya kuelekea Washngtone Dc ikafatia,wakijua watakaowapokea ni wale walowapanga wao.


Ila kumbe mkuu wa kundi hatari la Mafia nchini Marekani Max Arthur Merly alishamuwekea mtego akimtumia kijana wake jasusi hatari Agent Bray.


Ndani ya ndege kidume Zidu kiliketi pasina wasiwasi madaktari Wawili Stanley na dokta Julias na wasaidizi wao wakizidi kutazama usalama wa wagonjwa wao walolala vitandani pasina ufahamu tena wakitumia mashine za hewa ya Oxygen kupumulia....




Wagonjwa mahututi wanapandikiziwa unga wa madawa ya kulevya katika matumbo yao na kusafirishwa kuelekea nchini Marekani Butu akiwa mmoja happy wakisindikizwa na Zidu kijana katili aliyoko ndani ya usalama wa Taifa nchini Tanzania...


Pia tuliona habari hizi nyeti zinamfikia tajiri Merly Max Arthur mkuu wa mafia nchini Marekani haraka anaitisha kikao cha siri na kazi ile anamwachia kijana wake aitwaye Agent Bray kuhakikisha mzigo ule unafikia kwenye mikono yake je ATAFANIKIWA?!


Tusonge katika hatua ifuhatayo kuzidi kuburudika zaidi tiririka nayo


HATUA YA ISHIRINI NA NANE


*UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA WA WASHNGTONE DULLES*


Ndege binafsi ilomilikiwa na Raisi Bisau ilitua katika kiwanja kikubwa cha ndege Dulles mjini Washngton Dc nchini Marekani.


Kama ilivyo ada mlango ukafunguliwa na machela zilibeba wagonjwa haraka zikashushwa,madaktari maalumu waloandaliwa tayari walisogea kusaidia kupokea wale wagonjwa na kwenda kuwapakia katika magari yao ya wagonjwa.


Walipokamilisha safari sasa ya kutoka uwanjani kuelekea hosptal ikafatia....


Zilikuwa ambulance tatu moja ikipakia wagonjwa wa nne na hizo mbili zilipakia wagonjwa wa tatu wa tatu.


Ambulance ilokuwa mbele kabisa ndiyo alokuwepo Agent Bray kijana aliyekuwa na asili ya 'black America' akiwa ndani ya koti zuri jeupe la kidaktari nywele zake fupi alizichana Vizuri huku kidevu chake akiwa kakipendezesha kwa kuchonga ndevu mtindo wa 'O' macho yake akiyaficha kwa mawani ilomzidishia utanashati shingoni akitupia kipimo maalumu Cha kupimia mapigo ya moyo kiitwacho...........


Kamwe usingeweza kukubali kwamba yule si daktari kwa muonekano tu alokuwa nao tena alionekana Kama daktari mkuu katika jopo lile maalumu waloandaliwa kuja kuwapokea.


Ambulance ya pili walikwepo madaktari wale Wawili Silvester pamoja na Julias masikioni mwao wakiwa na earphone kwa ajili ya mawasiliano maalumu.


Na Ambulance ya mwisho alikwepo Zidu Katili yeye alipiga tisheti ilombana na suruali yake ya jeans na chini akitupia 'simple' Raba alipendeza hakika masikioni mwake alikuwa na 'earphone'alizounganisha na simu yake pembeni yake walikwepo madaktari wale walokuja kuwapokea wote lengo lao kuhakikisha hali za wagonjwa zinakuwa nzuri japo hata wangekufa kwao isingeleta shida yeyote.


Safari iliendelea gari mbili zile zikilifata gari ile ya mbele ambapo ndipo alipokwepo Agent Bray ambaye tayari dereva wake alishajua aneo analopaswa kuwapeleka.


Mbaya Zaidi Zidu akujua ni wapi miili ile inapopelekwa wala ilipo hiyo hospital ya Madison's Hospital ambayo ndio ilotumika kuwapokea wagonjwa mahututi na kuwafanyia upasuaji na kuwatoa hayo madawa kabla ya kusambazwa na mawakala maalumu waloandaliwa,kabla ya miili ile kuwekewa aina nyingine ya madawa na kusafirishwa tena Kama maiti ikitua jijini Dar watu maalumu uipokea kwa majonzi ivyo upita bila kukaguliwa.


Wakati safari ikiendelea ghafla simu ya Zidu ikaita kuangalia ni mheshimiwa Raisi haraka akapokea.


"Mmeenda wapi mbona amuonekani hapo uwanjani?!...."


"Ndo tupo njiani mkuu tushapokelewa?!."


"Unasemaje?!...mbona hapa madaktari kutoka Madison's Hospital wamefika hapo uwanjani awajawakuta."


Zidu akaduwaaa....


"Embu subiri muheshimiwa,...


Akamwangalia moja wa madaktari alokuja kuwapokea Kisha akamtwanga swali.


....Samahani daktari eti tunaelekea hospitali gani?!"


Daktari akageuza shingo kumtazama Zidu,akaachia tabasamu la kumtoa khofu.


"Madison's Hospital"


Daktari yule mmama unayeweza kukadiria miaka yake kwenye thalathini na nane au arobaini akajibu kwa sauti tulivu kisha akageuka kuendelea na shughuli yake.


"Mkuu wala usijali ni Madison's Hospital"


"Hapana umekosea fanya juu chini urudi uwanja wa ndege sasa hivi!,"


Raisi aliongea huku dhahiri alionekana kuwa na wasiwasi,pale pale Zidu akafikiria kuchomoa silaha yake amwelekezee dereva na kumpa amri ageuze gari ile anataka kuingiza mkono mfukoni alishtuka akitazamana na bastola ndogo wale madaktari wakiwa wamezishika Vizuri hapo Zidu akajua kumekucha ya kumepambazuka.


Simama yao,nyuso zao sasa zilibadilika,kwa haraka Zidu akajua wale si madaktari wa kawaida Kama alivyodhani awali.


Wana kingine zaidi ya udaktari.


Haraka akajitahadharisha kabla ya kutahadharishwa kuwa makini.


Akatulia tuli.


"Tulia hivyo hivyo usijiguse hata kujikuna tutausambaratisha ubongo wako..."


Yule dada aliyeonekana kuwa na tabasamu mwanzo aliongea kwa amri akiwa tayari kwa chochote.


"Mikono juu...."


Mwingine akatoa amri,Zidu alitaitika ikabidi atii haraka kijana mwingine akamsogelea na kuichukua silaha Kisha pale pale akapewa amri atoe mkono akachomwa sindano iloenda na fahamu zake....


No 29


Msafara ule wa gari za wagonjwa zilizidi kusonga mbele tayari Madamu Mery mwanadada hatari jasusi alisha mdokeza Agent Bray kilichotokea na walivyofanikiwa kumdhibiti Zidu kilaini tu....


"Congrats comred nilijua sikukosea kukuacha na huyo mtu!"


Agent Bray alimpongeza mwanadada yule,kwa kipindi hiki bilionea Max Arther Merly ndio aliyosadikika kulishika taifa la Marekani na yeye ndo alikuwa mdhamini mkuu wa chama tawala Cha American People 'AP' yeye ndo alopanga Raisi awe nani katika chama chake.


Na toka chama hiko kiingie madarakani Miaka 15 Raisi alimsikiliza yeye,alitumia wapelelezi maalumu na muhimu wa taifa Kama Kina Agent Bray,mwanadada Machachari Merry,na wengineo kwa mambo yake binafsi.


Arthur kazi yake kubwa ni usambazaji wa madawa ya kulevya duniani na kwa kuwa taifa lake lilikuwa kubwa akupata ukinzani wa aina yeyote na alikuwa na mawakala dunia nzima kundi lake likiitwa Mafia gengstar.


Miaka kibao nyuma wakala wake wa Tanzania akiwa ni waziri Patrick Bisau alituma mzigo wa ma bilioni,ghafla katika hali isiyo ya kawaida fedha zilichelewa kurejeshwa baadaye akasikia Bisau kachukua tiketi ya kugombea nafasi ya Uraisi na hata alipo ipata Bisau alimwambia pesa zake anazitumia katika kampeni akishinda Basi atazireuesha mara mbili yani na kiasi kile kile cha riba.


Kwa kuwa chama cha Patrick kilikuwa na nguvu Max alikubaliana naye,Bisau akapiga kampeni pa kuonga akionga mwisho wa siku akashinda tena kwa kishindo.


Kuwa Raisi Patrick kukamtia kiburi,Max alipoitaji hela yake akawa akizungushwa mwisho wa siku akatamkiwa wazi kutopatiwa hizo hela.


Mazoea ni mzigo kuutua ni ngumu , kwa kuwa Bisau alishazoea kazi ile ya magendo aliendelea nayo japo ni kwa usiri sana,kwa muda mrefu alitamani kuuza Marekani ila alishindwa kwa kuhofia mzigo wake kuingia mikononi mwa Max ila kwa kuwa taifa la Marekani soko lake lilikuwa juu akajipa muda wa kutengeneza mazingira.


Siku hiyo alialikwa kugawa vyeti kwa madaktari kadhaaa waliomaliza masomo yao,zoezi la ugawaji vyeti lilipokamilika Raisi akaomba aitiwe mwanafunzi mmoja punde kijana mmoja mchangamfu akaja.


"Ok unaitwa nani?!..."


"Madisoni Shemweta muheshimiwa!"


"Katika udaktari upo katika tahaluma gani?!"


"Upasuaji muheshimiwa Raisi"


Raisi Bisau akatabasamu,ndo mtu alokuwa akimtaka,kijana yule alikuwa ni yatima alolelewa na kusomeshwa na kituo Cha watoto yatima Cha Mkombozi, historia yake ya maisha pia ikamvutia Muheshimiwa Raisi.


"Nataka nikufungulie hospital nchini Marekani privet unaonaje?!"


Kijana yule akuamini ila Raisi alimpanga akapangilika,Madisoni akasafirishwa na kupitia balozi wa Tanzania nchini Marekani akafanyiwa mchakato wa uraia nchini Marekani,hospitali kubwa ilobeba jina lake Madison's Hospital ikajengwa na kuajiri madaktari wengi wakiwa wa Tanzania na wahindi.


Mpango ukakamilika.


Upasuaji ukawa ukifanyika pale watu wakawa wakipachikwa madawa ya kulevya na kusafirishwa Tanzania,hakuna alogundua hili kwa muda mrefu Bisau akawa akifanya kazi kwa uhuru huku Max akichunguza bila mafanikio.


Ila hakuna siri inayodumu milele ya mtu zaidi ya mmoja,siku ya siku Max akagundua siri ile naye kwa siri akakutana na dk Madison akampa fedha na kumpanga ampe Siri tofauti na ivyo angemuua Madison akaingia upepo,pesa akachukua na Siri akaitoa,mpango ukapangwa ukapangika,Max akaandaa vijana wake akiwemo Agent Bray wakawah uwanja wa ndege na kuwapokea kina Zidu baada ya kuondoka tu ndipo dk Madison alipowasili alipokuta wameondoka ndipo akampigia muheshimiwa Raisi Bisau na kumjulisha.


Raisi alichanganyikiwa,naye kwa haraka akampigia Zidu na kumuomba haraka arudi uwanja wa ndege.


Zidu akamuhaidi kufanya hivyo simu ikakatwa.


Zilipita dakika tano,Bisau akapiga tena kabla ya kukutana na sauti 'mteja unayempigia kwa Sasa apatikani tafadhali jaribu tena baadaye'.


Hata alipojaribu tena jibu likawa lile Lile.


Raisi akazidi changanyikiwa, ulikuwa Ni mzigo wa mabilioni...


Wasiwasi wake ulikuwa ni kwa mtu mmoja tu!....


Max Arthur Merly.


Akukosea,punde sms ikaingia katika simu yake haraka akaifungua kutaka kujua imetoka kwa nani.


Namba ilikuwa ni ya nje,


+1 859-962-3177


'Kwa kuwa umekuwa Raisi ukajua umekuwa Mungu wa dunia ukanidhulumu pesa zangu,Vizuri,ila usiangaike kutafuta mzigo wako pamoja na hawa Raia wako vyote kwa Sasa vipo chini yangu hii ni mwanzo rasharasha mvua inakuja....'


Ujumbe ule Raisi aliusoma zaidi ya mara tatu ila aukubadilika akapiga zile namba kabisa lakini pia azikupokelewa

Mwisho kwa hasira akaitupa ile simu na kuipasuapasua.


Ni Hasara kubwa sana aloenda kuipata!...


No 30


Hatimaye siri kubwa ilojificha kati ya bilionea mkubwa nchini Marekani Max Arthur Merly na Raisi Patrick Bisau tunaitambua,juu ya bifu lao la muda mrefu hatimaye Max Arthur Merly anafanikiwa kuiteka miili ya watu kumi ikiwa na madawa ya kulevya ndani,Bisau anachanganyikiwa kupata taharifa hizo je unadhani nini kiliendelea?!, Tusonge katika hatua ifuatayo nayo ni....


HATUA YA THALATHINI:


Haraka sana Raisi Bisau akamtwanga simu waziri mkuu wake Benson Sai na kuhitaji waonane haraka sana ikulu.


Muheshimiwa Sai alijiuliza ni nini kitakuwa kimetokea bila kupata jibu mwishoni akaona aende tu akasikie wito kwani ndo yalipo majibu ya maswali yake.


Dereva wale akampeleka mpaka ikulu,baada ya kusalimiana wakaingia katika chumba maalumu maongezi yakafuata.


Raisi Bisau alimweleza rafiki yake kila kitu kuanzia Madison alipompigia simu na kumtaharifu kutowakuta wagonjwa pale uwanjani,alipompigia Zidu na majibu alompa mpaka naye alipopigiwa simu na Max,hata waziri pia alichoka ila akakumbuka jukumu lake ni kuto kuonesha udhaifu na badala yake kumtia moyo kiongozi wake yule.


"Ni ku haidi tu muheshimiwa Raisi hakuna baya litakalotokea lazima Zidu ataukomboa mzigo wetu ni kijana ninayemwamini usijali kwa hilo muheshimiwa."


"Kwa hiyo kwa sasa yapaswa tufanyaje Sai"


"Tuwe na subira Muheshimiwa."


"Hapana Mimi na wazo."


"Wazo gani?!"


Sai akahoji akionekana kuwa na hamu ya kujua wazo hilo.


"Tumtume kk yeye pekee ndo anauwezo wa kurejesha mzigo pamoja na kumkomboa mumewe."


Kumbukumbu za waziri Sai azikufuta kazi alizowah kufanya Katarina,kumbukumbu zake ziliandikwa toka kuipatia uhuru Kinte,kupambana na mumewe Zidu uhodari wake wakaona wamtumie akauoneshe kwa bilionea yule.


"Haraka Katarina apigiwe simu nionane naye aingie kazini."


Mwisho Raisi akamaliza,waziri Sai akatoka sasa akiwa na matumaini.


**************


Mwili wote ulimsisimka,hatari ilishagonga katika kichwa chake si kawaida ya mume wake huwa akisafiri akifika salama umpigia na kumwambia mume wangu nimefika salama,ila safari hii mpaka muda huu akupigiwa.


Haraka aka amua akanunue vocha akatia katika simu yake akajiunga vifurushi vya nje akaitafuta namba ya mume wake anayoitumia Marekani akaipiga aikupatikana.


Akajaribu laini yake ya Tanzania pia jibu lilikuwa lile lile au simu imeisha chaji?!...


Hapana,alipingana na wazo hilo baada ya kugundua hata ndani ya ndege angeweza kuchajisha,alijua lazima mumewe atakuwa kaingia kwenye matatizo japo akujua Marekani kaenda kwa shughuli gani,pia alielewa mumewe alitumika kiuhalifu mara kibao alishamuomba abadilike bila mafanikio.


Wakati akiwa katika hali ya sintofahamu ghafla simu yake ikaita kuangalia alompigia ni 'privet namba' huku akiwa na wasiwasi akaipokea...


"Ni waziri mkuu Bisau hapa naongea unaitajika Ikulu na muheshimiwa Raisi kuna gari inakuja kukuchukua hapo nyumbani muda huu ivyo haraka sana jiandae ndani ya dk 5 uwe mbele ya Raisi"


Sauti ile ya waziri mkuu ikaitimisha,mwili wote wa Katarina ulimlegea jasho lilimtiririka akajua lazima mumewe kapatwa na matatizo je ni kafa?!,maswali mengi yakatiririka mawazoni,woga ukamtawala ila akajikaza haraka sana akaanza kujiandaa alipomaliza gari ikawasili akapanda Safari ya ikulu ikafatia.


Sasa kilikuwa ni kikao cha watu wa tatu, Raisi Bisau, waziri mkuu Sai na Katarina akiwa kaongezeka, Raisi hakuwa na budi kumsimulia kila kitu Katarina,mwisho akamueleza wazi kuwa kuitwa kwake ni kwa kazi moja tu,hata kuua ikibidi ila aokoe mzigo ikiwezekana na watu wale kumi wakiwa hai au maiti zao.


Akakabidhiwa paspoti na siku ilofatia ndiyo ilipaswa Katarina asafiri kuelekea nchini Marekani.


Kikubwa yeye alichofikiria ni kumkomboa tu mumewe katika mikono ya watu wale hatari.


Ni kazi ngumu itakayo yaweka maisha yake rehani


Roho mkononi!!!


Alilijua hilo, sekeseke analoenda kukumbana nalo alijua si la kawaida!


Ila je angefanyaje?!...


Mafia Ni kundi lililo ogopwa ulimwenguni.


Akaaga akiahidi kuifanya kazi Vizuri,akapewa baraka akatoka,tumaini kwa viongozi wale wa Taifa likarejea upya.


**********


Katika moja ya jumba la kifahari,jumba lenye ghorofa zaidi ya tano ndani pakiwa pamezungushiwa ukuta mkubwa wenye nyaya za shoti kamera za ulinzi na pakiwa na geti tatu zenye walinzi wa kutosha wenye silaha mabegani walojaza risasi.


Geti ya kwanza ikafunguliwa gari zile za wagonjwa zikaingia ndani pakiwa pamejengwa pakajengeka nyumba ndogo ndogo zikiwa pembeni zenye ghorofa moja mbili mpaka tatu yani kalikuwa Kama ka mtaa cha kitajiri gari zile zikaendelea kwenda hatimaye wakaingia geti la pili napo kulikuwa na walinzi maalumu pembeni pakiwa na banda la mbwa walobweka kwa ukali geti likafunguliwa wakaingia katika mtaa wa pili nao aukuwa tofauti na ule mtaa wa kwanza gari zile zikaendelea na safari hatimaye wakakutana na geti la tatu walinzi wakafungua na gari zile zikapita.


Mtaa huu ulikuwa tofauti na mtaa wa kwanza na wa pili mtaa huu ukuta wake ulikuwa mrefu zaidi kupita kuta za mtaa wa kwanza na wa pili pia ndani palionekana Kama pori miti ya matunda ilitawala si maembe machungwa migomba mbele kidogo wakaikuta bustani nzuri mbele ya bustani ile upande wa kushoto palikuwa na bwawa la kuogelea mbele nyuma ya bwawa Lile kulikuwa na jengo kubwa la ghorofa zaidi ya 50 ukitazama juu uoni mwisho wake.


Hili ndo jumba la bilionea Max Arthur Merly lililopo jijini Washngtone dc japo alikuwa na majumba Kama haya zaidi ya hamsini nchini Marekani,yani mitaa yake mwenyewe,pakiwa na hospital zake ndani maduka,masoko kwa kifupi katika mtaa huu wa tatu wa ndani hawakuruhusiwa kutoka nje,.


Japo mitaa hiyo miwili aliipangisha.


'Max Arthur Merly hospital'


Ambulance zilizimama mbele ya jengo ilo miili ile ikashushwa haraka na kuingizwa wodini.


"Haraka ipasuliwe na mizigo itolewa hakikisheni wanakuwa hai"


Agent Bray aliwa ambia madaktari walokuwa bize kuishusha miili ile.


Mwili wa Zidu kwa kuwa yeye alikuwa kalala akapelekwa katika chumba maalumu akafungwa kitandani kwa pingu maalumu akisubiriwa kuzinduka.


Tayari alikuwa ni mateka.....


Mwili wa Inspekta Butu na wenzake upasuaji ukaanza mara moja hali zao bado zilikuwa mbaya....


Merly Max Arthur mafia mwenye mtandao mkubwa hakupata tabu kugundua kutumwa kwa Katarina.


Alipotua tu uwanja wa ndege akaingia mikononi mwa wanausalama na taharifa akapewa.


Akacheka kwa kiburi akista ajabu upumbavu wa Rais Bisau na Mawazo mabovu ya kumtuma Mwanamke


Akaagiza Katarina apelekwe kwake akachanganywa na mateka wale kumi.


BAADA YA MWEZI MMOJA


Hali za mateka wale ziliendelea vizuri walipona kabisa Merly Arthur alishajua cha kufanya akawasiliana na shirika la habari la BBC na kuandaa kipindi Maalumu Cha watu wale kujielezea historia ya maisha yao.


Zidu na Katarina nao ili kuwa hai na mtoto wao Mdogo Sebastian aliyekuwa akademy Nchini humo kutodhuriwa ikawapasa waeleze ukweli wote Zidu akaeleza kutumika na Raisi kumtesa afisa wa Jeshi la Polisi Butu mbinu alizotumia kuiteketeza familia yake.


SEKESEKE likazaliwa nchini Tanzania watu wakaanza kuandamana wakishinikiza Rais Bisau sambamba na Waziri Mkuu wake kujiuzulu,


Jeshi likaingilia Kati kweli Bisau na Waziri Mkuu wakajiuzulu na kushtakiwa katika mahakama ya kimataifa na mwishowe wabaya wote Raisi Waziri Mkuu wake wakafungwa kifungo cha maisha.


Zidu naye alifungwa miaka mitano jela kwa kuwa alikuwa chini ya Rais ilikuwa lazima afate maagizo yake.


Inspekta Butu akarudi Kazini akipandishwa cheo na kuteuliwa mkuu wa Polisi ' IGP ' na Raisi aliyechaguliwa baada ya uchaguzi wa haki na amani ulosimamiwa na Jeshi la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania sambamba na umoja wa mataifa.


Hakika mafia japo lilikuwa ni kundi baya Ila kisasi chake kikaliletea mwanga Taifa la Tanzania.


Amani sasa ikatawala katika maisha ya Butu alopita yakabaki Kama historia ambayo asingeweza kuisahau katika maisha yake.


Alimshukuru Mungu tu kwa kuwa bado yupo hai tena akiwa mkuu wa Polisi huru katika taifa lake.


***************


MWISHO


SEKESEKE (ROHO MKONONI) - 4

   

Simulizi : Sekeseke (Roho Mkononi) 

Sehemu Ya Nne (4)




Aliyekuwa Inspekta wa Jeshi la polisi John Butu anafatiliwa kwa kila hatua pasina yeye mwenyewe kujua kama anafatiliwa,nyumba yake yote inategeshwa kamera za ulinzi,mambo ayaishi hapo hapana!,nje ya nyumba yake kandokando ya barabara anaonekana binti kichaa,


Na pia mtaa wa pili katika Restraunt moja anaweka makazi mjeda mmoja akiwa na kazi moja tu!....


Kumfatilia Butu kwa kila hatua....


Wakati huo Butu ana gida bia za kutosha ghafla anapata wazo,pale pale anainuka na kutoka,


Binti kichaa anamtaharifu kijana Isack akae sawa Butu anakuja usawa wake palepale Isack anamtaharifu Zidu anaye mwambia amtwange risasi naye atoweke ahakikishe aachi ushahidi,naye Zidu anakwea pikipiki kwenda eneo aliloambiwa!


SEKESEKE LILIANZIA HAPO! JE NINI KILIENDELEA?!...


tusonge katika hatua inayofuata kuzidi kuburudika!


HATUA YA KUMI NA SABA


Ile anataka kuichomoa bastola ghafla akasita baada ya kuona kamera katika jengo moja kubwa kando ya barabara..


"Usalama aupo vizuri watu ni wengi na magari pia ni mengi si vizuri kulianzisha nitalipaka matope jeshi letu!"


"Ina maana upo ndani ya Gwanda?!"


Zidu akamohoji


"Ndio kamanda"


Isack akajibu kwa majonzi


"ooh! Shit,usifanye chochote but endelea kuifatilia ujue inaelekea wapi"


"Sawa mkuu"


Kwa kuwa Isack alishaipita pikipiki ya Butu ikamlazimu apunguze mwendo,Butu akampita


Isack akaanza kumfata nyuma nyuma kwa siri sana ili hata asitiliwe mashaka!


***


Baada ya Butu kutoka tu kichaa yule wa kike alimsindikiza kwa macho baada ya kupotelea mtaa wa pili,akawasiliana na Isack,kisha akanyanyuka,akabeba pochi lake moja chafu na kuelekea kunapo geti,tena alificha uso wake kwa mikono kusudi kamera za pale getini zisinase sura yake.


Alipofika getini akaingiza moja ya funguo alizokuwa nazo,akafungua na kuzama ndani,alitembea haraka haraka juu ya tails zilizopo chini mpaka katika mlango wa nyumba ya ndani,akaingiza pia funguo,akafungua,ile kuingia akakutana na sebule nzuri,akaifata korido,chumba cha kwanza akasimama akashika kitasa akakizungusha kikamtwii,akazama ndani!


Hiki ndicho kilikuwa chumba cha Butu cha kulalia macho ya kichaa yule yakadondokea katika kabati,kwa hatua za taratibu akalifata,alipolifikia akatia funguo kabati likafunguka...


Kwa sekunde kadhaa akabaki akitumbulia macho ndani ya kabati lile!


Nguo zilikaa shaghalabaghala bila hata kukunjwa,binti kichaa akatingisha kichwa kwa masikitiko,akafungua pochi lake chafu cha ajabu ndani palikuwa na pakiti kibao za unga zilizofungwa kidogo kidogo katika vipakiti wenyewe uhita kete,akavitoa na kuvisukumia chini kabisa ya nguo!.


Baada ya kukamilisha zoezi lake,binti akabeba pochi lake lile chafu akatoka ndani ya chumba kile,akafunga mlango kama alivyoukuta,akaelekea getini akafunga,akatoweka mtaa ule,akiacha hatari kwa Butu!


***


Isack alizidi mfatilia Butu,huku akizidi kuwasiliana na Zidu!


"Naona anaelekea uwanja wa ndege mkuu!"


Akazidi kumjulisha!


"Ahaaa sawa,atakuwa anataka kwenda kuonana na wale watu wetu ngoja niwajulishe watoke pale kabisa,kingine badgal kashafanya yake ivyo akirudi home tu dogo hana uhuru!"


Isack alimuelewa Zidu alimaanisha nini,alimuaga akakata simu!


Safari iliendelea mpaka uwanja wa ndege wa Dia,Isack akapitiliza,kazi yake ilishaisha,maana kama angeendelea kumfatilia lazima Butu angemtilia mashaka na kitu hiki akikutakiwa!.


Butu alizikumbuka sura za wale wafanyakazi wa tano alowakamataga siku chache zilizopita.


Pia sura za wale waletaji wenye vipara zilinasa katika fikra zake.


Alienda mpaka mapokezi akajitambulisha na kutoa kitambulisho chake,akaomba apelekwe ofisi ya mkurugenzi wa uwanja ule akaelekezwa.Butu akaingia ndani ya lift kuelekea uko alipoelekezwa.


Baada ya kufika Mkurugenzi alimkaribisha Vizuri Butu akajitambulisha Kama alivyojitambulisha mapokezi

Mkurugenzi akahitaji kumsikiliza.


Butu akaomba 'list' ya wafanyakazi wote na picha zao,lengo pengine wale watano angewatambua angewabana lazima wangemfungulia kumjua mbaya wake,alitazama picha za wafanyakazi moja baada ya nyingine cha ajabu akumuona hata mmoja!...


"una uhakika hii ndo list ya wafanyakazi wako wote wa hapa earport?!"


Alimpachika swali mkurugenzi ambaye alimjibu ndo hao tu katika listi hakukuwa na wengine Butu akarudia kuwatazama tena,ila hakuona sura hata moja kati ya zile tano alizokuwa akizitafuta!


Maajabu!!!...


Utata!


Mashaka yakaanza kumvaa,hofu kumtanda!,akahitaji kuona list ya wasafiri wote walotua tar 4 ya mwez wa 4 mida ya saa tano akataja na aina ya ndege na namba zake,akapewa faili la siku hiyo akakagua,pia cha ajabu akuona picha kati ya watano wale alowakamata kabla ajaja kuwa achia kwa dhumuni la kuikomboa familia yake!...


Iweje picha zao zisiwepo?!...


Alizikumbuka sura zao fika,ila pale azikwepo!,nani anayemchezea?!, akajikuta akikosa raha,Butu akazidi kuchanganyikiwa akakifata kiti na kuketi!...


Macho yake yalikuwa mekundu,wakati akiwa kaketi pale ghafla simu yake ikaita,haraka akaitoa kucheki ni askari mwenzake Jonathan!,alokuwa akiisimamia kesi yake,haraka akaipokea ile simu...


Kwani alishakata tamaa ya kujua angefanya nini kwa kuwa kila upenyo auonao kuwa utamfikisha kumtambua adui yake unazibwa na kumuacha katika tafakuri kuu.


Ila kupigiwa na Jona kukamtia nguvu pengine alikuwa na habari njema kwake ambazo zingemuwezesha kumjua mbaya wake


Ni ule wakati Jonathan alipoamua kumpigia akapokea...


"kuna jambo nimeligundua tuonane muda huu kivulin bar tupate moja baridi,moja moto tuzungumze"


"Sawa!"


Palepale Butu hakakata pasina kupoteza muda akatoka ndani ya ofisi zile tayar kuianza safari,kivulini Bar.


***


18


Kamishna uchovu ulimchovya, alikuwa akisinzia ghafla akazinduliwa na mlio wa simu yake akaitazama alishtuka,ni baada ya kuona 'privet no,'


No za aina ile akuzipendaga kabisa ila akaamua kupokea Kama wajibu wake umtumavyo.


"Nurdin naongea sijui ni nani mwenzangu!?"


Kwa sauti ya utulivu,akijitahidi kutoweka mashaka Nurdin akazungumza...


"Nitambue kama raia mwema inatosha!"


Upande wa pili ukajibu kwa kiburi na dharau ya hali ya juu.


"Ok,nikusaidie nini?!"


Nurdin akaongea kwa hasira ni wazi akupendezwa na dharau za mtu yule


"Aliyekuwa askari wako mtihifu anauza madawa ya kulevya, Butu, kayaifadhi katika kabati lake la nguo chumbani,sasa kazi ni juu yako uamue kufatilia au upotezee juu yako mie nshakupa taharifa hiyoo"


Hapo hapo mpigaji akakata simu!


kamishna Nurdin akashusha pumzi ya kuchoka!


Ndiyo!,alichoka kwa lile aliloambiwa!, ila kama mkuu wa polisi akupaswa kupuuza chochote aambiwacho lazima achunguze mshtakiwa ahukumiwe!


Palepale akashika simu yake,tayari kumpigia Jonathan kijana aliyemwamini kati ya vijana wake wote!.


Upande wa pili baada ya Zidu kukata simu akaachia cheko kuna watu wengine alihitaji kuwa taharifu wakaweke mtego nyumbani kwa Butu ili tu akitolewa wasambaze habari zake!


Waandishi wa habari,...


Alijua polisi wangeweza kuficha jambo lile kusudi kutolipaka matope jeshi lile ila kama waandishi wangeliripoti lazima Butu angeishia pabaya.


Akatabasamu tena palepale akaichukua simu yake tayari kwa kuwasiliana nao,awapange.....


Jonathan akiwa katika kikao alimueleza kila kitu Butu,juu ya kutekwa kwa mama yule,ambaye mumewe ndiyo wao waliyo muua!,wakajaribu kuyaunganisha matukio haya mawili wakapata picha!,kwamba Silivestar familia yake ilitekwa baada ya yeye kugundulika ni msaliti,akajitoa muhanga kufa ili familia yake ipate kuwa huru!,ila sasa je Silvestar ilikuwaje mpaka kutoa siri za watu hao?,je walitapeliana?,ni watu gani wanaukaribu gani na Silvestar?!,bado maswali yakawa mengi kwao!,ila ghafla simu ya Jona ikaita...


"Nakuomba wewe na wenzako mje hapa ofisini mara moja kuna dharura imetokea"


Ikabidi kikao kifungwe,haraka Butu akarudi nyumbani kwake pasina kujua kinachoenda kumtokea.


Inspekta Jona na wenzake wakarejea ofisini!


"Bebeni silaha za moto tuelekee katika cruzer haraka twende kwa Butu,maaskari wale sasa wakawa wakishangaa,ila wakatii amri,wakaingia ndani ya gari ya polisi,Jonathan na kamishna Nurdin wakiwa mbele,huku Patrick,Paul na Isack wakiwa nyuma ya bodi,Jona akaliwasha gari tayar kuelekea kwa ins Butu!


***


Butu alikuwa sebuleni mwake akipitia pitia gazeti ghafla akasikia sauti ya ka kengele cha mlango akasimama na kwenda kufungua,alishtuka kumkuta mkuu wake na walokuwa maaskari wenzake!


"Tunahiji kukagua nyumba yako Butu!"


Nurdin alisema,butu alibaki katika mshangao pasina kuelewa nini kinachoendelea,yote yale Zidu aliyaona,katika simu yake maafisa wale wa polisi wakaingia na kuelekea moja kwa moja chumbani!


"Tunakuomba ufungue kabati!"


Butu bila ubishi pasina kujua kipi kinaenda kutokea akaingiza funguo na kufungua kabati,nguo zikaanza kutupwa chini,punde kete zile za madawa zikaanza kutolewa,palepale Butu akawekwa chini ya ulinzi, akavikwa pingu, na kutolewa nje! Cha ajabu nje waandishi walikwepo wa kutosha aikujulikana walitaharifiwa na nani!,picha zikafatia...


Butu akaingizwa kwenye gari safari ya kwenda kituoni ikafatia!,akiwa chini ya ulinzi mkali!


Tena akiwekwa na wale walokuwa chini yake kicheo!...


Walompigia saluti na kumuheshimu....


Sekeseke linaanza kuya andama maisha ya aliyekuwa inspekta wa jeshi la polisi John Butu,pasina kujua anategeshewa madawa ya kulevya katika kabati lake chumbani sasa yupo chini ya ulinzi wa jeshi la polisi ni nini kitakachoendelea?!,


Butu atasalimika kweli?!,tusonge katika hatua hii kujua kilichoendelea!


*HATUA YA KUMI NA TISA NA ISHIRINI*


Habari za kukamatwa kwa aliyekuwa afisa wa jeshi la polisi zilizagaa,vyombo vya habari vyote vilielezea,watu mbalimbali waka andamana kushinikiza askari yule kupewa adhabu kali!.


Wakati hayo yakiendelea Mkuu wa polisi Igp Gerald Uwiyo aliketi ofisini kwake,kichwani kwake alikuwa na mawazo sana,alimkubali sana Inspekta Butu alishtushwa na habari alizozipata,hakuziamini kabisa na alijua lazima kuna mchezo kijana yake yule atakuwa kachezewa,si bure,haraka akachukua simu yake na kumtwangia Cp Nurdin,Nurdin alimuelezea kila kitu,toka kupigiwa simu na mtu alojitambulisha kama raia mwema na kumueleza juu ya kuwepo kwa madawa ndani ya kabati la Butu,walipofatilia na kufanikiwa kuyakuta!.


"Mlikagua cctv camera?!"


"Hapana mkuu hatukufanya ivyo!"


"Ndo kosa mlilokosea,haraka sana uchunguzi uanze mara moja wapatikane hao washenzi wanao mchafua huyu kijana wangu!"


"Sawa mkuu!"


"Ok,ntakutafuta acha niongee na mh Waziri naona anantafuta!..."


Palepale Igp Uwiyo akakata mawasiliano na kamishna akampokelea waziri!


"Umeona habari inayoendelea kwenye vyombo vya habari juu ya kijana wako?!"


"Ndiyo mkuu,lakini kwa hisia zangu Butu kasingiziwa awezi kuwa muuzaji kuna mchezo..."


"Usitake kunifanya nika amini kwamba Raisi alikosea kukuteua mkuu wa polisi,kijana wako kakamatwa na ushahidi,kalichafua jeshi zima la polisi bado unataka kumlinda eti ufanyike uchunguzi nina chokuomba toa tamko katika vyombo vya habari kulahani tabia hiyo na pia uhaidi adhabu kali kwa askari huyo masikio ya wananchi wote yapo kusikiliza serikali itachukua hatua gani,narudia tena apewe adhabu kali iwe fundisho kwa watu wengine hii inaonesha hata siri ya kuipoteza familia yake anaijua..."


Igp alishtuka kwa amri ile,lakini ilipaswa aifate japo moyo wake ulimuuma,haraka kama alivyoambiwa akahitisha mkutano wa waandishi wa habari aka laani kitendo kile cha Butu na kuiomba mahakama itoe adhabu kali kwa mshtakiwa!...


Hakika sasa maisha ya Butu yalikuwa hatarini!


Roho mkononi!!...


Jeshi lilimtenga,marafiki walimtenga,alifikishwa kituoni akatupwa rumande na kesho yake akapelekwa mahakamani...


***


Mahakama ilifurika watu,wengi wakitaka kujua ni nini hatma ya polisi yule aliyekutwa na madawa nyumbani kwake.


Hatimaye akapandishwa kizimbani ,akasomewa shtaka lake la kukutwa na madawa ya kulevya alipoulizwa alikubali kukutwa nayo japo alikana kujishughulisha na uuzaji,alisema wazi aliwekewa kimtego,utetezi wake ukakosa nguvu akahukumiwa miaka 35 na kulipa faini,wengi walifuraishwa na hukumu ile,.


Butu mwenyewe binafsi alishangaa kesi yake ilivyopelekwa haraka haraka mpaka kuhukumiwa kwake,hapakuwa na uchunguzi,wala nini,sasa anaelekea gerezani,hakuwa na ndugu wala familia wa kumpigania,hakuwa na rafiki wala hata mpz wa kumfariji,akaingizwa katika karandinga tayari kwa kwenda kuya anza maisha mapya ya gerezani.


*'NA AHIDI NITATOKA MR X SITOKUACHA HAI,SAFARI HII UMESHINDA ILA SAFARI NYINGINE UTOSHINDA NASEMA'*.


Huku akiwa kaji inamia,ndani ya karandinga lile Butu alijiwazia safari ikiendelea.


***


*SURA YA TANO*


*LANGO LA JEHANNAMU:*


Lango la geti kubwa likafunguliwa na wanajeshi walovaa nguo za magereza,karandinga lile lililobeba wafungwa likapita.


Lango likafungwa!...


Karandinga lile ilitembea kama dakika kumi na tano katika njia ndogo huku pembeni ya njia hiyo pakiwa na miti,ilikuwa ni mfano ya hifadhi ya msitu ndo wameingia.


Hatimaye baada ya mwendo ule wa dakika kumi na tano na ushee hatimaye walifika mwisho wa kale ka njia mnyohofu ,mbele yao palikuwa na jengo kubwa sana ambalo juu kidogo ya mlango palikuwa na maandishi makubwa mekundu yalosomeka

'GEREZA LA SEGEREA'.


Mbele ya jengo lile palikuwa na bustani nzuri ambayo katikati yake iliwekwa bendera ya taifa,palikuwa na uwanja mkubwa!.


Hapa ndipo wafungwa waliposimama mistarini pale ilipowabidi kukutana,na jengo lile ndipo zilipokuwepo ofisi ya mkuu wa magereza na askari wake,.


Gari likapakiwa eneo maalumu la maegesho wafungwa wote ambao walikwepo takribani kumi na mbili wakashushwa na kuswagwa kuingia ofisini!.


Walifikishwa mpaka ofisi ya mkuu wa magereza,wakapewa mavazi mekundu yalokwepo katika mfumo wa ma ovaroli,pamoja na namba za miaka yao watakayoishi gerezani pale!.


Butu akipewa namba 35 ikiwa na maana ni miaka 17 na miezi sita,kwa hesabu za kifungwa!,


Mkuu wa magereza kimuonekano alikuwa ni mzee kichwa chake chote kilijaa mvi,ila ukakamavu ulinyonya uzee wake wote,akaonekana ni mtu katili,asiye na roho ya huruma hata chembe,hakuwa mtu wa kucheka hata na askari wake,kugomba ilikuwa hulka yake!...


"Na sikia kuna polisi hapo ni yupi huyo Mshenzi?!".


Mkuu yule wa polisi akauliza kishari,wala Butu akuangaika kumjibu,mpaka askari mmoja alipo muonesha kwa kumnyo oshea kidole!.


"Huyu anao nekana ni jeuri apelekwe kwanza lango la jehanamu akakae huko masaa 24 kesho ndo tutampangia mahabusu kati ya triple a,b au c sawa?!"


"Sawa mkuu!"


Wafungwa wale wakatolewa sasa kupelekwa katika vyumba vya mahabusu yao!,kesho ndo wangeanza kazi rasmi!.


Baada ya wafungwa wale 12 kutolewa,mkuu yule akashika simu yake na kuipiga!.


"Zidu nishamuona mtu wako,masaa 24 ya awali ataishi na siafu nyoka,na wadudu wote watambahao waumao,hana siku mbili atakufa tu kwa mateso tutakayo mpa hapa ndo segerea!".


"Safi sana ancle,kijana mdogo anataka kupambana na watu wakubwa mwache ajionee".


Zidu aliongea kwa furaha,akakata simu!.



Kwa upande wa Butu si kwamba akulijua lango la kuzimu,yeye ni askari,sifa ya jengo lile alilijua,jengo hilo lilitumika kama adhabu kwa kumuua muhalifu aloshindikana,yeye anapelekwa huko,kwa uhalifu gani aliokuwa nao?,kwa kosa gani alofanya yeye mpaka kustahili kupewa adhabu kubwa kiasi kile?!....


Tumaini sasa la kuishi lilimyeyuka, roho mkononi,ilikuwa ni nadra mtu kuingizwa kule na kutoka,hakukuwa na sakafu,palikuwa na mashimo ya nyoka wakali,siafu wa kutosha,mashimo ya panya wakubwa ambao si wakawaida na juu kabisa kulikuwa na popo walotambulika kwa jina la popo mdonoo.


Unajua kwa nini walipewa jina hilo?!


Butu alijua sababu na mbaya zaidi chumba hicho kilichojengwa kwa umbo la duara,kilikuwa ni giza tupu.


Hatimaye ka mlango ka dogo kama cha kuku ila cha chuma kakafunguliwa akapewa amri aingie, akatii, kakafungwa!.


Ghafla baada ya kuzama ndani likasikika yowe!.....


Kunanini?!



Sekeseke lina ya andama maisha ya Inspekta wa jeshi la polisi John Butu roho mkononi,hatari ya kuyapoteza maisha yake anaiona kabisa,anasekwa ndani ya gereza la Segerea mbaya zaidi anajikuta katika selo ijulikanayokwa jina la lango la jehannamu,selo hiyo uki ingizwa aina stori ya kutolewa ukiwa mzima,kwanza ndani kumetawaliwa na kiza,hewa hafifu,na wadudu waumao,je Butu atasalimika ndani ya hayo masaa 24?!


Tusonge katika sehemu hii ya ishirini na moja


HATUA YA ISHIRINI NA MOJA


Baada ya Butu kusukumiwa ndani,kamlango kale kakafungwa,Butu aliachia yowe akijua wazi sasa ndo anaenda kukutana na mateso makali,alipokewa na kiza kikali,nuru ya mwanga aikupata kuwepo ndani ya eneo lile,pua zake zikanusa harufu kali,tena harufu mbaya,ni mizoga ya watu ilooza ghafla akahisi mwili ukianza kumchoma choma,akujua ni saa ngapi alivua lile ovaroli akitoa wadudu wale aina ya siafu waloanza kumtembelea,


Wakati akiwa bado ana angaika ghafla akadonolewa usoni,hakupata tabu kugundua kuwa wale ni popo mdonoo!


Akujua afanye nini,ashike wapi,kati ya mwilini au usoni,ghafla akahisi akidonolewa mguuni,panya nao walisha anza yake.


Ndani ya dakika tano mwili wote ulimvimba,akajikuta akishindwa kuvumilia kuendelea kusimama akaenda chini,hapo ndipo wadudu walipoendelea kumshambulia vizuri,kadri muda ulivyozidi kwenda ndivyo nguvu zilivyozidi kumuisha na hali ilizidi kuwa mbaya!.


Ambacho hakutaka kusahau ni swala la kusali sala zake za mwisho,kumkabidhi Mungu mwili wake!.


Imani kwamba ataendelea kuishi ilishamtoka kabisa.


***


TRIPLE C JAIL


Eneo lingine ndani ya gereza lile la segerea juu kabisa ya lango paliandikwa Triple c,gereza hili la segerea lilijengwa kwa matabaka,na kila tabaka lilijitegemea katika makazi yake,kula kwao,na hata maaskari wake,japo mkuu wa gereza alikuwa ni mmoja,na katika kila tabaka walizungushiwa ukuta mkubwa,lango la kuzimu lilikwepo upande wa triple c,watu walokwepo katika tabaka hili ni wale waloshindikana,majambazi sugu,watu makatili au wenye kesi za kusta ajabisha,kuuana humu ilikuwa kawaida,hata maaskar wao walikuwa nunda vilevile na kila mara walikuwa na mbwa waloijua kazi yao vyema!


Kutoka triple c,kulikuwa na triple B,huku walikwepo watu wa kawaida,wezi wa kuku,wakabaji,wauaji wa kutokukusudia,wezi wa mtandao,na aina nyingine ya wahalifu wadogo wadogo,huku walikwepo askari wakawaida na tabaka la mwisho ni triple A,hawa ni class A,Vip wafungwa walikula chakula kizuri,walilala pazuri waliangalia Tv,walisoma magazeti,hawakupewa kazi ngumu,wengine hawakupewa kazi kabisa,huku walikwepo viongozi wakubwa wa dini,viongozi wa serikali,wasanii,huku ndipo ilipaswa aswekwe Insp Butu naye ndo alijua ivyo ila kitendo cha kupelekwa lango la kuzimu kukamtilia shaka.


Ndani ya ofisi ya mkuu wa magereza Dunga,mbele yake alikwepo askari wake mtihifu,dakika 15 zilishakata askari yule akiwa mbele ya mkuu wake pasina kusemeshwa chochote,dharau ya aina gani hii!,Dunga akijifanya yupo bize na game katika simu yake mguu kauweka mezani,kijana kasimama wima kikakamavu mbele yake,akumjali mpaka alipo kosea na mchezo kuisha ndipo aliposhusha miguu yake chini akaweka simu yake chini na kumwangalia askari aliyekuwa mbele yake!.


"kruta nenda triple c,namuhitaji Manzua haraka ofisini kwangu"


"Sawa mkuu!" Kijana yule akajibu kikakamavu na kujinyanyua kidogo ishara ya kutoa heshima akageuka na kuufata mlango.


Akatoka!.


Alienda mpaka lango la Triple c,akamnong'oneza mlinzi naye akarudi zake,mlinzi akachepuka kuelekea zilipo selo apatikanapo mtu huyo!...


***


Ndani ya selo moja alionekana kijana mmoja alojengeka kimazoezi akiwa kamkamata vyema kijana mwenzake kamnyongea ukutani,kimya kilitawala sauti ya mwamba yule pekee ndo ilokuwa ikisikika.


"Mali ya manzu huwa aipotei, ulinidhulumu uraiani ukajua nimefungwa utanufaika pekee yako wapi sasa leo nakuua kwa mkono wangu sheitwan wewe"


Jamaa yule alomkaba mwenzake aliongea kibabe akizidi kumnyonga mtu yule,punde maaskari wakawasili,ndipo mtu yule alipo muachia yule alo mnyonga hata ivyo hakuwa hata na punje ya uhai tena!"


"Manzu umeua tena?!"


Askari yule alokuja alio ngea kwa ukali,huku akimfata manzu gobole kalishika kwa mbele yani eneo silaha inapo chomokea.


Polisi wengine watano wakiwa nje langoni,silaha wakiziweka tayari!.


Askar yule ambaye ndiye alokuwa langoni na kuambiwa Manzua anahitajika kwa mkuu,alilifikia njemba lile na kuinyanyua gobore lake ile analishusha kichwani kwa sugu,njemba ikapangua na kuudaka ule mkono akauzungusha ukalia kaaa,kilichofatia ni yowe,punde askari wale watano wakazama kumweka kati,ila bila kutegemea jamaa alikuwa mwepesi akafurukuta akimzawadia kila askari teke lake aliye enda kumdondokea mfungwa waliyekuwepo ndani mule,...


Wote wakasimama na kukimbilia gobore zao ila kabla awajafanya kitu ikasikika nje sauti!


"Acheniii!"


Tena ikiwa sauti kali na ya amri maaskari wakasitisha jambo lile, wafungwa wote wakasimama! Kumpa heshima mtu yule,


"Nilituma niitiwe huyu mtu matokeo yake mnampiga ndicho nilicho tuma?!"


Mkuu wa gereza akauliza huku akimwangalia yule mfu alouwawa muda mchache ulopita!


"Lakini mkuu kausika na mauaji tena!"


Askari yule alopigwa wakwanza akajibu huku akishika mkono wake,


"Sicho nilicho tuma mfatilie,chukueni huo mwili mkauzike,jembe langu nifate!"


Mkuu yule akaongea kwa kiburi huku akimwangalia Manzua,aloachia tabasamu,akamfata mkuu wake nyuma,yeye kuwapiga maaskari tena maaskar watukutu ilikuwa kawaida,kuua wafungwa kwake wala akujali...


Maaskari walishindwa kumuua kwa kuwa alipendwa sana na mkuu wao,ivyo kumuua ni kujitafutia kukosa kazi na ikiwezekana kuishia pabaya.icho kikampa uhuru bedui lile kufanya atakalo,hakukuwa na wa kumbambaisha!.


Alifika ofisini kwa mkuu wa magereza akapewa ishara aketi maongezi yakafatia


"Manzu kuna kijana kwa saivi yupo ndani ya lango la kuzimu,sijajua kama atapona,ila akipona kesho atakuwa katika chumba chako mpe mateso uwezavyo hata ukimuua sawa tu!,hii ni kazi ya kwanza nakupa na sitegemei kuniangusha sijawah kukupa kazi kabla,na ukfanikiwa hili ntakupa mwanamke mzuri wa kukidhi haja zako!..."


Dunga akaweka tuo,kwa furaha jamaa yule hakuwa na la kujibu aliishia tu kufurahia,akapewa ruksa aondoke zake,gerezani kupewa mwanamke ilikuwa ni zawadi kubwa alikuwa na miaka zaidi ya mitatu ajawah kukutana na mwanamke,yeye hakuwa na muda mrefu sana gerezani...


Aliomba Mungu huyo maiti wake atoke mzima aje afie mikononi mwake!,japo akujua ni mtu wa aina gani!


BUTU ATASALIMIKA LANGO LA JEHANNAMU,AKITOKA ATAPONA KWENYE MIKONO YA MANZU?!.


TUONANE KATIKA HATUA IFUATAYO KWA MWENDELEZO


RIWAYA YA KIJASUSI&UPELELEZI


SEKESEKE(ROHO MKONONI)


MTUNZI:ZUBERI MARUMA22


WHATSUPP:0759427653


No:0673999120

0624408343


22


Aliyekuwa inspekta wa jeshi la polisi John Butu anaingia katika sekeseke la hatari!


Dalili za kuyapoteza maisha yake zinaonekana dhahiri shahiri!


Anategeshewa madawa ya kulevya anakamatwa anahukumiwa na kuswekwa lupango,mbaya zaidi anaingizwa ndanh ya selo ijulikanayo kama lango la jehannamu,hakuna historia ya kuingia huko na kutoka ukiwa hai naye anajikuta katika mateso makali je atasalimika kweli?! Tusonge kuzidi kuburudika zaidi!


HATUA YA ISHIRINI NA MBILI


Kiza kilitanda ndani ya macho yake,kumbukumbu kwa mbali zikaanza kumjia!.


Akajaribu kufumbua macho yake, yalikuwa mazito kana kwamba yakigoma kufumbuka ila hatimaye yakafumbuka.


Akajaribu kuvuta kumbukumbu ni wapi hapo alipo,kumbukumbu azikumsapoti,zikagoma kabisa,ila alijua muda ule ni usiku kutokana na kiza kizito,kichwa kilikuwa kizito kwa maumivu makali.


Akatuliza akili!,hapo hapo sasa ndipo kumbukumbu zilipoanza kumrejea maumivu makali ya kausweka moyo wake,akataka kujaribu kusimama pale alipojilaza akashindwa,akatamani hata kukaa pia kwake ikawa ngumu.


Akang'amua hata mwili wake pia umekufa ganzi.


Hapo ndo akachoka kabisa!


Akujua amelala kwa muda gani pale,tumbo liliunguruma kwa njaa angekula nini na uwezo wa kutafuta kwa kipindi hicho kigumu cha kutumikia adhabu alopewa na nchi yake!


Maumivu ya kichwa yalizidi kumgonga,kizunguzungu kikali kikamvaa,ganzi aloipata ilimsaidia kwani hakusikia maumivu ya kung'atwa na siafu wala panya,ikabidi aendelee kulala akiwa kakata tamaa kabisa! na alitamani kufa kwenda kuungana na familia yake kuliko mateso yale mpaka muda ule akujua anapambana na kina nani!,ila alijua ni mtandao mkubwa na ni watu wenye uwezo mkubwa kumzidi hata yeye.


***


Katika jumba moja la kifahari la Zidu alitumihalo kufanyia baadhi ya mikutano yake ya siri,kuhifadhia pia mateka wake,juu ya ghorofa ya tatu katika varanda ya nje kwenye makochi walikaa watu wa tatu,kilikuwa ni kikao cha siri,Zidu akitoa mrejesho wa kazi yake kwa mheshimiwa Raisi na waziri mkuu wake.


"Yule kijana kwa sasa yupo magereza na nimeshaongea na mkuu wa gereza lile mtu yule afe tena kwa mateso makali!"


Walimpongeza sana Zidu kwa kazi aloifanya,alipo yeye hapakuwa na kinachoharibika,waliendelea na maongezi yao wafanyakazi wa jumba lile waka wa andalia chakula wakala hatimaye wakaaga!.


***


BAADA YA MASAA 24


NDANI YA OFISI YA MKUU WA MAGEREZA:


Mkuu wa gereza la Segerea Dunga aliketi katika kiti chake,macho yake yakiwa katika kompyuta yake,mdomoni kulijaa mabuyu alokuwa akiyatafuna na mbegu kuziweka kwenye meza yake,buyu hizo alichukua katika kakopo kadogo!,ambapo alikanunua kakiwa kamejaa na sasa ndo alikuwa anamalizia,macho yake yalidondokea katika saa ilokwepo ukutani hapo ofisini kwake akatabasamu,zilisalia dakika kumi kukamilika kwa masaa 24 toka kuletwa kwa Butu pale,akashika mkonga wa simu yake na kuweka masikioni akabonyeza namba kadhaa simu ikaita!


"Naam afande"


Upande wa pili ukaitika kwa sauti nyororo ya kike,


"Niitie askari yeyote hapo mapokezi"


"Sawa afande,.." Binti yule akajibu na kukata simu


"Mudy unaitwa ofisini kwa mkuu"


Pale pale binti akamlenga mtu alomtaka yeye,na kijana huyo binti alo mpendekeza akijua bosi ka muhitaji akajinyanyua na kuelekea ofisini kwa mkuu wake!.


"Kusanya hizi mbegu ukazitupe kwenye dustbeen hapo nje uje hapa!"


Kijana yule akazikusanya zile mbegu bosi wake alizokula na kwenda kuzitupa kisha akarejea kwa mkuu wake!.


"Nenda kamtoe yule mfu lango la jehannamu kama ni Maiti mwacheni aozee huko,ila kama ni mzima mkamtupe triple c tumeelewana?!"


"Ndiyo mkuu"


Yule askari alijibu huku akionesga wasiwas wa waziwazi usoni mwake,aliushangaa ukatili wa mkuu wake ila kwa kuwa tayari ilikuwa ni amri ilikuwa lazima akaitelekeze.


Akawashtua maaskari wenzake, wakaelekea lango la jehannamu wote walijua wangekuta maiti kwani mtu yule toka awekwe kule akula chochote.kunywa wala kuonja,tena akiwa ndani ya mateso makali!


Leo wamkute hai?!


JE BUTU ATAKUWA MZIMA?! TUONANE KATIKA SEHEMU IJAYO KWA MWENDELEZO


RIWAYA YA KIJASUSI&UPELELEZI


SEKESEKE(ROHO MKONONI)


MTUNZI:ZUBERI MARUMA22


WHATSUPP:0759427653


No:0673999120

0624408343


23


Aliyekuwa inspekta wa jeshi la polisi John Butu bado maisha yake yapo hatarini,ndani ya masaa 24 anafungiwa ndani ya chumba kijulikanacho Kama lango la jehannamo huko apewi chakula, anakutana na wadudu wa uchungu wa kila aina,baada ya masaa 24 kuna mtu anatumwa na mkuu wa magereza akamfate,akimkuta hai apelekwe triple c,akikutwa maiti aachwe tu huko huko,kijana yule alotumwa akifatwa na wenzake wanaenda mpaka kwenye selo ile wanafungua mlango na kuchungulia wana cho ona kinawashtua je wameona nini?!


Tusonge kupata mwendelezo


HATUA YA ISHIRINI NA TATU


vijana wale wakafika,mmoja akachuchumaa na kufungua kale ka mlango kisha akamulika kwa kutumia tochi iliyokuwepo mkononi mwake,akuamini alichokiona,Butu alikuwa kakaa kitako tena akionekana mwingi wa mawazo,.


"Yupo hai,haya toka haraka"


Askar yule aliwa ambia wenzake muda huo huo akimpa ishara Butu atoke kule,Butu alisimama,akajitahidi kupiga hatua akaenda chini,mwili wote bado ulimuuma na tena ulikosa nguvu ikabidi atambae alipotoka akanyanyuka wakamsaidia kumshika mpaka selo,wote walimuonea huruma ila ndo ilikuwa amna namna,walimfikisha katika selo triple c,lango likafunguliwa akasukumiwa ndani!.


Wafungwa wakampokea kwa furaha akiongozwa na nyapara alokwisha pewa kazi na mkuu wa gereza kumtesa kijana yule ikiwezekana hata kumuua amuue tu.


Kabla akijafanyika chochote kengele ya msosi ikagongwa wote wakatoka, Butu akijitahidi kutembea kwa kushika ukuta asidondoke,naye akachukua sagani yake na kujipanga katika msitari,hatimaye zamu yake ikafika naye akawekewa chakula.


Mpaka muda huo hapakuwa na mfungwa alotaka urafiki na yeye,wengi wakisema hakuna urafiki kati ya askar na mfungwa.


"Chezo yule fala si ndo alinikamataga akanipiga sana na kunisweka rumande,akasimama mahakamani kama shahidi mi nikafungwa sasa leo kaingia kwenye kumi na nane zangu ataisoma namba"


Ilisikika sauti ya mfungwa mmoja ikimnong'oneza mwenzake,na palepale akampa sahani yake amshikie taratibu akamfata Butu pale alipo!


"Hoya we fala unanikumbuka!, ulipokuwa kitengo ukajiona afisa utopatwa na matatizo leo umeingia kwenye 18 zangu utaupenda utawala!"


Mfungwa yule alokuwa na namba 15 katika ovaroli lake akaongea kwa kiburi,ila kwa jeuri Butu akawa anakula,alijua mambo kama haya yatajitokeza ivyo alijua jinsi ya kukabiliana nayo,alowatia kule ndani ni wengi hivyo alijua visasi ni vya kutosha,bila uwoga,bila kumtazama usoni yeye akaendelea kula,jamaa akazidi kukasirika.


"Yani wewe boya naongea na wewe nawe waendelea kula nadhani ujanijua vizuri wewe".


Mtu yule akapiga hatua kadhaa na kumfikia Butu akamnyang'anya ile sahani ilikuwa kosa,ndani ya masaa 24 ajala,akajikuta hasira zikimpanda nguvu zikamjia akajiinua akapiga hatua ya kwanza hatua ya pili akamdaka kijana yule namba 15 kola ya ovaroli lake akamgeuza na kumzawadia ngumi moja ya usoni,jamaa akaachia chakula,butu akakidaka.


"Weweeeeee!, tena na usije ukajaribu tena kuingia katika vita yangu sitosita kukuua,usije ukajaribu tena mpumbavu wewe"


Butu alimpa onyo huku akimbana mdomo tena kwa nguvu,alipo maliza akamsukumia kule,akageuka sahani yake mkononi akarejea alipokuwa ameketi awali.


Tukio lile Nyapara Manzua aliliona,hapo akatambua ukorofi wa mtu yule!.


Si goigoi kama alivyodhani,baada ya chakula wakarudishwa katika selo zao.


Butu alienda akatafuta eneo akaketi,akaegemea ukuta,akaji inamia akiyapa nafasi mawazo kukiandama kichwa chake.tayari alishaua viumbe visivyo na hatia,na siyo ivyo tu amejikuta akiwa gerezani kwa kosa ambalo akulifanya,wakati akiendelea kuwaza si ndo Manzu akazama ndani,kwanza alishtuka kumkuta Butu kakaa sehemu yake kwake ikawa kashapata sababu,akamfata akiwa mwingi wa jazba.


"We kijana nani kakuruhusu ukae hapo nadhani ujataka kumjua Manzu ni nani sasa leo utanijua vizuri."


Manzua akapayuka kwa hasira huku akipiga hatua ndefu kumfata pale alipo,Inspekta Butu akanyanyua kichwa chake,akawa tayari kumsubiria mtu yule kweli Manzua alifika,akanyanyua mkono wake aloukunja ngumi akiupeleka alipo Butu,kijana akakinga mkono wake mkono wa Manzu ukapiga mkono wa Butu,ndani ya sekunde ile ile Butu akajinyanyua na kukaa tayari,Manzu akapiga hatua tatu ndefu za chapchap nyuma,akaunyanyua mguu wake kwa uwepesi kumuendea Butu,ila kijana akawa tayari kashaliona lile teke akalipangua kwa mkono wake,sambamba na kurusha konde zito shavuni kwa Manzua likampata sawia,manzu aka achia mguno wa maumivu,ila akajikaza akataka kujaribu kuirudisha usoni Butu akainama ngumi mbili zikapiga hewa wakati alipoji inua akarusha konde jingine la tumbo Manzu chini...


Wakati hayo yakiendelea wafungwa walikuwa wakishangilia kupigwa kwa manzu,aliwaonea sana,si wafungwa pekee hata maaskari nje walichungulia wakifurahia kitendo kile.


Kila pigo Manzu alilopiga aliambulia maumivu,mdogo wote ulitapakaa damu...kelele za ua,ua,ua,ua zilizagaa,


ITAENDELEA

SEKESEKE (ROHO MKONONI) - 3

   

Simulizi : Sekeseke (Roho Mkononi) 

Sehemu Ya Tatu (3)





Inspekta wa jeshi la polisi John Butu anapokea barua ya kuamishwa kazi,jambo hilo anapingana nalo na kuamua kuandika barua ya kuacha kazi kabisa je unadhani nini kitaendelea?!


Tusonge katika hatua nyingine kuendelea kuburudika zaidi


HATUA YA KUMI NA MOJA:


Tayari akili yake ilishagubikwa na ukungu wa kukurupuka,


Akupenda hata kuchukua wasaa angalau dakika moja na ushee aidha kutafakari kile akifanyacho.


Tabia hii kila mara ndo ilo mfanya ajutie kile aamuacho kwanzia kumuua yule mwandishi,kumuua huyu alo mjua kama mr x na pia kuandika barua ya kuacha kazi,akaikabidhi kwa bosi wake,akuishia hapo akapiga

saluti muinuko,na kutoa kofia yake ya polisi akaiweka mezani,palepale akageuka na kuuendea mlango,hata mkuu wake alipo muita akuangaika kugeuka,alisha amua,na Butu kawaida yake akiamua kaamua huwa arudi nyuma.


Askari wenzake walishtuka kumuona katika hali ile,kengele ya hatari ikagonga katika vichwa vyao,ila hakuwa na muda wa kuwaeleza kilichotokea,akaingia ndani ya gari yake kuelekea kwake


Huku nyuma kamishna Nurdin alishika simu yake akapiga namba kadhaa akaweka simu masikioni simu ikaita...


"alooh!"


Upande wa pili ukapokea.


"Mkuu ni kwamba Butu kaacha kazi baada ya kumpa barua ya uamisho!"


"Ushawatangazia wenzake juu ya jambo hilo?!"


"Hapana mkuu!"


"Vizuri na usiwatangazie,haraka sana na kuitaji ofisini kwangu tujadili hili!"


"Sawa mkuu"


Palepale simu ikakatwa,


Pasina kupoteza muda kamishna akajinyanyua na kuelekea nje,ambapo aliingia ndani ya gari yake tayari kuelekea alipopajua yeye.


***


Katika jumba moja la kifahari,maeneo ya Tmk Vetenary,eneo aliloishi Inspekta Butu ilisimama pikipiki akashuka mtu ambapo baada ya kutoa element akavaa kofia la sweta lake lililo muwezesha kuficha sura yake akaanza kuliendea geti la nyumba ile alipofika akaingiza mkono wake ulovalishwa gloves katika mfuko wake wa jeans akatoka na funguo aina ya orlando akaziingiza katika kitasa cha geti akafungua haraka akazama ndani!


Alipofika mlango wa ndani akafanya vivyo hivyo,


Safari yake ikaanzia sebuleni alipopanda juu ya meza ya kioo,akuogopa kuivunja,akategesha kitu juu pembeni ya taa,kitu icho kidogo mfano wa kifungo ilikuwa ni ngumu kuonekana kwa urahisi!.


Alipomalika alishuka na kuelekea upeuni palikuwa pembeni kidogo na eneo lile la kupumzikia,eneo hili la kulia,akapanda juu ya meza kubwa ya mbao,pembeni ya taa akategesha kile kitu chake,sasa akashuka na kuelekea vyumbani,alifanya ivyo ivyo katika kila chumba pamoja na bafuni,sasa akarejea sebuleni peyuni,juu ya meza palikuwa na kompyuta mpakato alimaharufu kama laptop,akaiwasha, katika soketi,ikawaka sasa ikaitaji namba za siri,mtu yule akatabasamu akatoa flash na kuchomeka, akabonyeza bonyeza ajuavyo yeye laptop ile ikafunguka,akaanza kufanya alojua yeye,wakati akiendelea katu akujua nje mwenye nyumba aliwasili.


Alishtuka kukuta pikipiki nje ya nyumba yake,haraka akashuka na kuchomoa pistol yake,kwa mwendo wa haraka tena kwa uangalifu akaanza kunyata kulifata geti akafungua taratibu na kuzama ndani!,akaanza sasa kusonga mbele mpaka kwenye mlango wa nyumba ya ndani,akashika kitasa na kukikunja taratibu ghafla akaufungua na kuzama ndani!


Ile anaingia akapokewa na teke,kwa kuwa lilikuwa ni la ghafla lilimtupa pembeni pistol nayo ikamponyoka,


Mtu yule kwa haraka akauwai mlango na kutoka,


Butu akukubali kumuacha akainuka akaifata bastola yake akaiokota na kuuwai mlango akaufungua na kutoka nje,akaanza kurusha risasi ila mtu yule alikimbia kwa mwendo wa zig zag mpaka kulifikia geti,Butu bado alimmiminia risasi zilizo mkosa kosa,mtu yuld akafanikiwa kufungua mlango wa geti lile akaiendea pikipiki yake akavaa element na kuiondoa kwa kasi,Butu naye akukubali alipofika nje akapanda gari yake naye kuanza kuifukuzia ile pikipiki!.


Mfukuzano uliendelea ila mtu yule alikuja kumpotea makutano ya tazara,akumwona tena hata alipofika buguruni na kujaribu kuuliza akupata ushirikiano mwisho akaamua kurejea kwake,huku kichwani akiwa na mawazo mengi,je mtu yule ni nani!, ndo Mr x au mfuasi wake?,alikuwa anafanyaje kwenye kompyuta yake,aliwaza sana,kichwa kilimuuma kwa mawazo,alipofika kwake akaiendea kompyuta yake na kuifungua,akukuta cha zaidi,akaangaza angaza macho kule ndani pia akuona cha tofauti,akaiendea friji akatoa chupa kadhaa za bia akaweka mezani akachukua glasi na kuanza kuzigida,wakati akiendelea kunywa ghafla akapata wazo,haraka akajinyanyua na kuiendea pikipiki yake,akapanda na kuiondoa,safari yake iliishia katika duka liuzalo kamera za cctv,wakafanya maongezi akalipia,mafundi wakaingia kwenye gari yeye akaongoza mbele na pikipiki yake safari ya kuelekea kwake ikafatia,aliamua kwenda kufunga kamera za ulinzi!...




Inspkta John Butu ana amua kuacha kazi,ni baada ya kupewa barua ya uamisho,


Anarejea nyumbani,ila anashtuka kuikuta pikipiki nje ya nyumba yake kuingia anamkuta mtu akichezea kompyuta yake,mtu yule asiyemfahamu anafanikiwa kumponyoka,Butu anaamua kwenda katika duka la kamera anachukua mafundi na kuwaleta nyumbani wana anza kutegesha kamera za ulinzi katika jumba lile tusonge kujua kilichoendelea...


HATUA YA KUMI NA MBILI


Watu wale wa cctv kamera walifanya kazi haraka haraka,wakiweka nje kwenye mlango kamera mbili sebuleni wakaweka ukutani na katika kila chumba,wakaunganisha na kompyuta zoezi lote likakamilika,awakuweza kuzitambua kamera zilizokuwa ndani ya kidude cha taa juu ya paa la nyumba ile


'Kazi sasa ishakamilika,boya yeyote atakayeingia humu nitamuona tu!'


Butu akawaza.


***


Upande mwingine zilipo ofisi za mkuu wa polisi 'igp' ili ingia gari,maeneo ya maegesho akashuka kamishna Nurdin,akaanza kupiga hatua kuelekea lilipo jengo la ofisi ya mkuu wake yule,njiani alipigiwa saluti.


"Mkuu yupo?!"


Alimuuliza katibu muhtasi wa mkuu wa polisi ambaye alitingisha kichwa kuafiki!


"Kasema ukija nikuruhusu ukamuone karibu kamishna".


Nurdin akujibu kitu akageuka na kuelekea upande ulipo mlango ambao juu kulikuwa na maandishi inspekta jenerali wa polisi 'I G P' alipofika akagonga,akashika kitasa akakizungusha na ku usukuma kidogo kwa ndani mlango akapata upenyo,akaingia,akaurudishia mlango kama alivyoukuta.


Alimpigia saluti mkuu wake,akampa ishara aketi Nurdin akamtwii!


"Lete habari,kijana kakataa uamisho?!"


Mkuu wa polisi alotambulika kwa jina la IGP STEVE jina lake kamili ni Julius Steven akauliza,kabla Butu ajajibu mlango ukafunguliwa na binti ambaye ni katibu muhtas wa Steve


Akaruhusiwa akaingia...


"Mkuu nikuletee nini?,chai,maziwa?!"


"Mletee Arabic ni mpenzi sana wa kahawa huyu jamaa,"


"Na kashata bila kusahau!".


Kamishna Nurdin akadakia wote wakaachia kicheko,


"Na wewe mkuu?!"


Binti akamgeukia bosi wake akamuhoji akimtupia tabasamu mwanana....


"Mi maziwa na bajia"


"Bajia,bagia?!"


Binti akamsahihisha...


"Ivyo hivyo ujuavyo binti!"


Igp akajibu kwa tabasamu binti yule

mrembo akageuka tayari kwa kuondoka.


Akapiga hatua kuufata mlango huku nyuma akisindikizwa na macho ya maafisa wale.


Baada ya kutoka ndipo maongezi yao yaliposhika hatamu.


"Yah,kijana kaacha kazi,kasema kuliko ahame Dar bora aache kazi bado anahitaji kulipiza kisasi!"


IGP akatingisha kichwa kwa masikitiko!


"Na vipi kuhusu upelelezi wa kesi yake?,ulo mkabidhi faili anasemaje?!"


"Amna chochote mkuu kesi ile ni ngumu tena inaonekana hao majamaa wana mtandao mkubwa sanaa"


"Kivipi iwe ngumu na mara ya mwisho ulinambia huyo 0759427653 mlimtia nguvuni?!"


"Mkuu nasikitika kukwambia yule mtu alikuwa siyo na Butu alimuua kimakosa hawa majamaa waliunganisha tu namba,"


"Unataka kunambia yule mlomkamata alikuwa ahusiki kwa chochote?"


Kabla CP Nurdin ajajibu mlango ukafunguliwa na binti yule akaingia mkononi akiwa na visahani viwili kimoja kikiwa na kashata kingine bagia,kashata akakiweka karibu na Nurdin kile cha bagia akakiweka karibu na Steve kisha akatoka.


Nurdin akaendelea....


"Yule mtu alikuwa ahusiki kwa chochote mkuu ni kosa tu lilitendeka na Butu ajui kama mimi najua hili!"


Igp Steve akashusha pumzi nzito,akakuna kichwa chake...


"Sasa nani atakuwa anahusika kwa haya yote?!"


Akamtupia swali,ikawa sasa zamu ya Nurdin kutafakari,kimya kikatanda baina yao,wakati kila mtu akiwaza lake mlango ukafunguliwa yule binti akaingia mkononi akiwa na vikombe viwili vya udongo,kimoja kikiwa na kahawa,kingine kikiwa kimejaa maziwa akaenda kuwaekea,


"Asante Muni kaendelee na kazi"


Igp akamshukuru mfanyakaz wake,


"Huyu kijana anapitia katika wakati mgumu sana,namuonea huruma kwa sasa tumuache afanye anachotaka zoezi zima likimalizika ndipo tumrejeshe kazini!"


Igp akatoa wazo lake,


"Sawa mkuu nitafanya ivyo,"


"Kingine mwambie huyo anayeisimamia kesi yake kila atakachogundua asisite kumwambia,mpaka hao washenzi walio iteketeza familia ya chombo cha dola waipate posho yao,iliniuma sana"


Hatimaye Igp alitoa ruksa kwa Butu kuendelea na kazi akiwa nje ya jeshi,japo Butu akutakiwa kuwambiwa chochote.


Ni wazi jeshi zima la polisi liliumizwa kwa alichofanyiwa.


***


SURA YA TATU


TEMEKE MIKOROSHINI


KATIKA JUMBA MOJA LA KIFAHARI


Katika chumba kimoja ndani walikwepo watu wa tatu,mwanamke mmoja ambaye anaweza fikia umri wa miaka 37 na wanaye wawili mmoja wa kike akiwa kama na miaka 17 huyu alionekana ndo mkubwa na wa pili wa kiume huyu miaka yake kumi na mbili,wote walikuwa katika hali ya majonzi,humo ndani walipokwepo hawakuwa huru!.


Walifungiwa!.


Chakula waliletewa na watu walojifunga nyuso zao,kutoruhusu sura zao zionekane,kuoga walioga humo humo,walitekwa na awakujua walitekewa nini,awakuambiwa chochote,siku ya tatu sasa ilishapita toka kutekwa kwao!


Awakujua wapo wapi kwani waliletwa wakiwa wamefungwa macho na walipofunguliwa wakajikuta katika chumba kile,hawakupewa mateso yoyote!...


Siku hii kama kawaida mlango ulifunguliwa,wakaingia watu wa tatu wote wakiwa wamefunika nyuso zao,ilikuwa ni mapande ya usiku!...


Kama saa moja na nusu hivi


"Leo mnarudi kwenu!"


Mmoja kati ya watekaji wale alizungumza,akawapa ishara wenzake wakawafunga vitambaa katika nyuso zao,wakawaswaga mpaka nje wakawaingiza kwenye gari safari ya kutoka katika jumba lile ikafatia...


Gari ile ilienda mwendo mfupi kabla ijaingia lami na kuchukua uelekeo wa tazara maghorofani,ikaelekea mpaka buguruni,safari yake ikaishia Tabata Matumbi ikaingia katika barabara ya vumbi na kuacha lami,ikakatiza mitaa kadhaa na mwisho ikasimama katika nyumba moja nzuri ya kifahari pia,watu wale wakafunguliwa vitamba usoni mwao,hawakuamini!,ni kweli mbele wali iyona nyumba yao,


"Mama tumewa achia huru atujawatesa wala kuwa ekea alama yoyote,usiripoti polisi kwa chochote juu ya utekaji huu na wala msiende polisi kuripoti chochote kama mnapenda kuendelea kuishi! Sawa?!"


Dereva akamta adharisha mama,alotingisha kichwa kukubali!


"Mkienda kinyume na ichi tulichowaomba tutawachukua na Safari hii amtaishi Kama mlivyoishi hapo awali nadhani mmenielewa"


"Sawa baba tumekuelewa atutaripoti chochote"


Mama yule akajibu kwa unyenyekevu


Dereva akampa ishara kijana mmoja akafungua mlango mama na wanaye wakashuka na gari ile ikaondoka,wali isindikiza kwa macho mpaka ilipoishia ndipo walipopiga hatua kuifata nyumba yao!.


Pamoja na yote wakati ile gari inaondoka mama yule alifanikiwa kuzikaririsha namba za gari lile.


Furaha sasa ilitanda ndani ya mioyo yao,wakalifikia geti na kubonyeza kengele wakasubiri wafunguliwe,geti lilionekana kufungwa kwa ndani!.


No 13&14


Ni katika mazingira ya kutatanisha familia moja ilitekwa,mama na wanaye wawili,wa kike na mdogo wake wa kiume,walikaa kwa muda wa siku tatu wakaachiwa tena wakapelekwa mpaka kwao,wakafunguliwa vitambaa usoni kabla ya kushuka dereva alimuonya mama yule kutoripoti chochote polisi,mama yule alikubali,ila alikaririsha namba za gari lile,je ni watu gani wale,kwa nini walitekwa na walitekwa na watu gani?! Tusonge


*HATUA YA KUMI NA TATU NA YA KUMI NA NNE*:


Walisubiri kwa muda punde hatua za mtu akikimbia kwa ndani zikasikika,


Na ghafla ikasikika kuguswa kwa geti kama kufunguliwa kwa komeo lililopo ndani,geti likafunguliwa.


"Heeee mamaa!"


Akatoka binti mrembo akamkumbatia yule mama kwa furaha!.


"Salima mwanangu nilishakwambia kabla ujafungua geti uwe una uliza kwanza ni nani?!,we unakimbilia kufungua geti je angekuwa mtu mbaya?"


Mama alianza kuteremsha lawama baada ya kumwachia m

yule binti alotoka ndani ya ile nyumba sasa wakawa wakiingia ndani


"Sawa mama nimesikia,mlienda wapi nawapigia ampatikani mjini ikawa mjini kweli!"


Wakati wakiingia ndani yule binti akaendeleza stori


"Yani we acha,kwanza baba yako yupo?!"


Mama akajibu sambamba na kumpachika swali binti yule.


"Hayupo! toka ile siku mlo ondoka ajarudi nikajua mko wote! "


"Eti?!, Unasema?!"


Mama yule akahoji kwa mshangao pasina kuamini kile alichokisikia.


"Baba ajarudi toka juzi mama,na watu wengi wamekuja kumuulizia wengine wakiwa wafanyakazi wenzake"


"Jamani mume wangu atakuwa salama kweli?!"


Mama aliuliza huku machozi yakimmwagika,walifika sebuleni mama akatangulia kuweka simu yake chaji,ilishazima toka ile ile siku ya kwanza walipotekwa.


"Ukwenda polisi kutoa taharifa juu ya upoteaji wetu?!"


Mama akazidi kumdadisi yule binti...


"Sikwenda mama,mi nilijua mtarudi!"


"Hapana Salima,hali kama hii siku nyingine ikitokea katoe taarifa kituo cha polisi kikawaida atuwezi kusafiri bila kukuaga,ungekaa utusubiri mpaka lini tungekufa je?!"


"Kwani ni nini kilichotokea mama?!"


Ikabidi sasa yule mama aanze kumsimulia mfanyakazi wake kilichowapata!...


"Siku ile nilipokea sms kutoka kwa mume wangu,sms hiyo ilisema kuna gari itakuja kutuchukua hivyo nijiandae basi nikamwambia Martha na Bray wajiandae kweli gari iliwasili tukatoka na kuingia,ile tumeshakaa vioo vikapandishwa palepale tukawekewa silaha tukafungwa macho atukujua tulipopelekwa,tulikuja kuambiwa tushuke tukapelekwa tulipofunguliwa vitamba tulikuwa ndani ya chumba,ndipo tulipokaa uko,chakula tuliletewa huko huko,kila kitu tulifanyia humo humo"


"Mh! Poleni kumbe mlitekwa mama?!"


"Ndio na nahisi pengine watu wale walihitaji ela kwa mume wangu ,ila kitendo cha kunambia naye toka juzi ajaja kinanitia shaka sana"


"Baba atakuwa kwenye matatizo mama lazima ukaripoti polisi!"


Brayson mtoto wa wakiume wa yule mama akashauri,kabla dada yake ajadakia


"Hapana mama!,unakumbuka yule dereva alivyosema?!,ukienda polisi watatuua"


Sasa kila mtu akawa akisema lake kwa kuwa simu ilishapata chaji kidogo mama akaifata na kutafuta namba za mumewe akazipiga!,lakini azikupatikana.


Kwao huu ukawa mtihani mwingine, maskini mama akujua kama kwa sasa yeye ni mjane mumewe alishakufa tena kwa kupitia mikono ya aliyekuwa inspekta wa jeshi la polisi John Butu


Ni baada ya kumuhisi mtu yule kwamba ndo 'MR X' ilikuwa hivi!....


SURA YA NNE


UPANDE WA PILI WA SHILINGI


IKULU


Kilifanyika kikao cha siri katika chumba kimoja cha mikutano ndani ya Ikulu ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Ndani walikwepo watu wa tatu,walionekana kuzama katika maongezi yao yalokuwa nyeti


"Mheshimiwa mtukufu Raisi nimemgundua msaliti atoaye siri zetu ni mr Silvester huyu ndiye alimpigia simu afisa wa polisi kwa kutumia namba za siri 15551 na kumjulisha juu ya ule mzigo wetu na pia akamjulisha juu ya mbinu za uokoaji tulizopanga kuzitumia..."


"Saadash Zidu kazi nzuri na nijijua ndani ya masaa 6 utakijua kirusi kilichopo katikati yetu,msaliti wetu utamjua,chakufanya ahukumiwe kifo mara moja!"


Mheshimiwa Raisi akajibu kwa furaha kwani alishajiuliza sana ni nani aliyekuwa na udhubutu wa kuunguza ishu yake polisi mpaka kukamatwa kwa vijana wake na alijua lazima atakuwa mtu wake wa karibu na sasa alishamjua.


"Na si mimi nitakaye muhukumu lah!"


Akashtushwa na kauli ya kijana wake yule alomuamini zaidi ya kitu chochote!


"Bali?!"


Waziri mkuu naye akahoji,Zidu akacheka kabla ajajibu swali lile


"Huyo huyu ampaye habari zetu ndiyo atakayemwangamiza tena kikatili sana"


"Kivipi sasa?!"


Kwa shahuku Raisi Bisau akahoji Zidu akaachia tabasamu tena ,


"Nahitaji niwaoneshe kwa vitendo!"


Alijibu huku akiwa katika tabasamu jepesi,akashika simu yake na kupiga namba kadhaa,akaweka sikioni akasubiri kwa sekunde kadhaa simu ikapokelewa...


"Mzee tunakikao cha siri na muheshimiwa Rais,pamoja na waziri mkuu ivyo tunakuomba nawe ufike hapa katika chimbo langu huku matumbi"


Kumbe kijana yule alikuwa akiongea na Raisi Patrtick Bisau pamoja na waziri mkuu Benson Sai,Zidu alikuwa ni mkuu wa usalama wa taifa ndo mmiliki wa ile namba 0759427653 aliyo iunganisha toka kwenye simu ya Kijana alotambulika kwa jina la Zuberi,na mzigo ule ulikuwa ni wa Raisi pamoja na waziri mkuu wake,ila uliratibiwa na Zidu mwenyewe,Silvestar yeye alikuwa mfanyakazi ofisi ya Raisi akupendezwa na kazi ile kwa siri sana akatafuta namba za siri na kumjulisha inspekta Butu kabla ya kugunduliwa!


Baada ya kumaliza kuongea na mtu yule sasa Zidu akawaomba wakuu wale wa nchi waelekee kwake wakamsubiri huyo kijana


Pasina msafara watatu wale wakaingia ndani ya gari Zidu akiwa dereva Safari ya kuelekea Tabata Matumbi ikafatia.


Dakika kumi tu waliwasili wakawa aKimsubiri Silvester tena kwa hamu kubwa sana.


Pasina kujua alichoitiwa Mr Silvester aliwasili katika jumba ilo la siri la Zidu,akatoa heshima kwa viongozi wale wa nchi akaambiwa aketi!,bila wasiwasi akaketi,Zidu akamuomba simu yake Sili pasina kujua akampa,


"Namba za mke wako umezisevuje huku?!"


Zidu akahoji kishari sasa sura ilibadilika,Sili akajua hapa si salama tena!


"Kuna nini wakuu?!"


Silvestar akahoji kwa wasiwasi!


"Utajua,wewe si msaliti sasa dawa yako ndogo,sema namba ya mkeo umesevuje humu?!"


"Wi..fe" Mzee wa watu akajibu kwa woga huku akishindwa kujizuia kutetemeka!.


"ha ha ha eti wife,sawa hii hapa!..nimeiona"


Zidu akatuma meseji aloijua yeye,kisha akaifuta na kumrejeshea mwenyewe simu yake,muda ule ule akatoa simu yake na kuwapigia watu wake...


"alooh,Isack naomba muelekee nyumbani kwa Silvestar mke wake na watoto watatoka muwapandishe kwenye gari muwafunge macho wasijue mnapowaleta muwalete huku matumbi katika nyumba yangu ya siri sawa?"


Upande wa pili ukaitikia sawa,kweli baada ya kama nusu saa gari ile iliwasili,wakiwa katika chumba kingine kupitia dirishani Silvestar aliona familia yake ikishushwa na kuingizwa katika chumba kingine!


"Ili kuikomboa familia yako lazima wewe ujifanye mimi!,mimi nitawasiliana na huyo mpumbavu wako na kuhitaji kuonana naye then wewe utaenda kama mimi,utapokea malipo yako ya usaliti kwetu ndipo tutaiachia familia yako ukienda kinyume na hichi wewe na familia yako yote tutaiteketeza katika visima vya mamba,hata mifupa yenu aitoonekana"


Hapo ndipo Mh Rais na waziri mkuu wake waliuelewa ukatili wa Zidu k,hapo ndipo walipo muelewa vizur zaidi,palepale Zidu akatoa simu na kumpigia Butu akahitaji aonane naye kivulini bar usiku wa siku hiyo,


Akawaita vijana wake kadhaa na kuwapa kazi wampeleke hapo bar usiku,na ndivyo ilivyokuwa Sili aliamua kufa kuitetea familia yake,usiku aliingizwa garini mpaka Kivulini walipofika dereva akampigia simu Zidu kumtaharifu kuwa amefika,Zidu akaomba wawili wamsindikize mpaka atakapoketi ndipo waondoke,ikawa ivyo,Silvestar akakamatwa Butu akimjua ndiye mr x wake! na kwenda kumwangamiza kikatili pasina kujua.


Sasa ndo wakaiachia familia yake.


Walipofika nyumbani wakakuta hali ya sintofahamu kutoka kwa binti wa kazi Salima.




Zidu anafanikiwa kumgundua mheshimiwa Silvestar kuwa ndiye aliyempa taharifa afisa wa jeshi la polisi John Butu na kumwezesha kukamatwa kwa unga wa madawa ya kulevya,haraka kikao kinafanyika ikulu na mwisho muheshimiwa Raisi Bisau anatoa amri Silivestar kuuwawa,Zidu anahaidi kumtumia huyo huyo Butu kufanya kazi hiyo na ili linatendeka baada ya kuiteka familia yake na kumwambia ili aiachie huru lazima akajikamatishe kwa Butu kama yeye Silivestar anakubali ili kuikomboa familia yake,je nini kitaendelea?! Tusonge katika hatua inayofuata:


HATUA YA KUMI NA TANO:


Usiku ule hakukuwa na aliye kuwa na hamu ya kwenda kulala,mpaka inatimia saa nane wote walikuwa macho,sebuleni pale wakijadili kipi cha kufanya,japo waliwasha tv ila hakukuwa na aliyefatilia kilichokuwa kikiendelea katika runinga ile,woga uliwatawala!


Bi Glory kwa vyovyote vile alijua lazima mumewe atakuwa kwenye hatari,kama si kupoteza maisha.


Bray alimsisitizia mama yake pakipambazuka aende kituoni,akaripoti,tena kituo kikuu cha polisi,japo Martha alimpinga mdogo wake akisisitiza onyo walopewa na yule dereva,ila bi Glory akakata shauri itakavyokuwa na iwe,atawezaje kukaa kimya bila kwenda kuripoti kupotea kwa mume wake?,na alijua fika akienda polisi pia ni lazima aeleze ukweli,kwamba nao pia walitekwa...


Akazima tv na kuwataka watoto wake wakalale,naye akaelekea chumbani kwake kulala


Kwa kuwa walichelewa kulala pia walichelewa kuamka,Bi Glory kabla ajafanya chochote akachukua simu yake na kumpigia shemeji yake,yani mdogo wake na mume wake,ndo ndugu pekee alokuwa amebakia kwa upande wa mume wake,akamuomba afike nyumbani,kwa kuwa hakuishi mbali kweli alifika akamuelezea,shemeji yake alotambulika kwa jina la Michael alimpa pole sana shem wake!,akamtoa khofu na kumwambia lazima waende kituo cha polisi...


Asubuh ile ile safari ya kuelekea kituoni ikafatia.


***


KITUO KIKUU CHA POLISI


Kamishna Nurdini alikuwa kakaa ndani ya ofisi yake kakasirika,kila dakika aliguna,mdomo aliukunja,si muda mrefu alikuwa ametoka kumgombeza kijana wake Inspekta Jonathan,ni muda mrefu sasa toka amemkabidhi kesi ya afande Butu aloipoteza familia yake,ila mpaka muda ule alotoka kuongea naye kijana yule hakuweza kugundua kitu chochote juu ya kesi hiyo.


Kwa upande wa Jonathan alitoka akiwa na hasira ofisini kwa mkuu wake.


Alikumbuka wao wa nne yani yeye Butu,paul na Andrea walishamuua alosemekana ndo mmiliki wa ule mzigo,walimteka kivulini Bar usiku ule wa kampeleka katikati ya msitu na kumuua kikatili sana!


Cha ajabu baadaye Butu akaja kumwambia mtu yule siye,bali ni yule alokuwa akiwasiliana naye kwa namba 15551 na kumpa maelezo,mpaka muda ule akujua mtu yule ni kwa nini aliamua kuuvaa uhusika wa adui yao na kukubali kufa siri yake ikibaki moyoni,aliwaita wenzake Paul na Andrea ofisini kwake na kuwa ambia jinsi mkuu alivyotoka kumgombeza!


"Unadhani tutafanyaje afande na yule mtu atumjui bora tungeijua hata familia yake..."


Ni wakati wakiendelea kujadili upande wa mapokezi akiwa binti Fatma waliwasili,bi Glory na shemeji yake,walikaribishwa wakaketi Fatma aka anza kuandika maelezo yao!


"Ok! Naweza kuwasikiliza!"


"Eleza kila kitu shem usifiche kitu hapa ni usalama wa raia ivyo toa wasiwasi"


"Ni kwamba siku tatu zilizopita nilitumiwa meseji na mume wangu alinambia nijiandae mimi na wanangu kuna gari inakuja kutuchukua,nikijua ni sapraiz nika wa andaa wanangu punde nikasikia honi nje nikamuaga mfanyakazi nasi tukatoka nje tulikuta gari tukafunguliwa mlango tukaingia,ile tumeingia vioo vyote vikapandishwa juu wale watu wakatubadilikia na kutufunga usoni,sijui walitupeleka wapi,ila tulikuja funguliwa macho tukajikuta ndani ya chumba kimoja,tuliletewa chakula mule,tulikaa siku tatu mpaka jana tulipoambiwa tupo huru tukafungwa macho na kurejeshwa nyumbani ambapo watu wale walitupa onyo kuripoti polisi ila tulipofika ndani na muulza Salima habar za mume wangu akanijibu toka tuondoke naye ajarudi,tukimpigia apatikani sijui mume wangu atakuwa kapatwa na nini!..."


"Salima ndo huyo mfanyakazi wako?!"


Fatma akahoji,


"Ndiyo!"


"Watu hao walowateka walishawapiga,au kukupigeni picha au hata kuwapa simu muongee na mume wako?!"


"Hapana awajawahi!"


"Mumeo anaitwa nani?!"


"Silvestar Emanuely!"


"Anafanya kazi gani?!"


"Yupo ofisi ya Raisi ikulu pale"


"Je ulishawahi kumsikia mumeo akigombana na mtu? au unamjua adui yeyote wa mumeo unaye dhani anahusika katika utekaji wenu,au kupotea kwake?!"


"Hapana afande,"


"Ok,nahitaji picha yake,"


Bi Glory akaingiza mkono kwenye pochi yake akatoa picha ya mume wake na kumkabidhi afande yule,


Fatma alizicheki kwa muda kisha akasimama...


"Naomba mnisubiri..."


Akalinyanyua lile kalabrasha aliloliandika,akapanda nalo juu mpaka katika ofisi ya kamishna,katibu muhtas akamruhusu Fatma akagonga na kuzama ndani!


Alimkuta kamishna bado kanuna,akampa lile faili,kamishna akaanza kulisoma...


"Mh!," Nurdin akaachia mguno akishangazwa na maelezo yale,hakika maelezo yale hayakuwa ya kawaida hata chembe!...





Bi Glory ana amua kwenda polisi kushtaki kupotea kwa mume wake,pia anaelezea juu ya kutekwa kwao,yeye na watoto wake wawili Bray na Martha,walimkuta mapokezi afande wa kike alotambulika kama afande Fatma,afande yule alokuwa na cheo cha u koplo,aliandika maelezo yao kisha akaelekea na faili ofisini kwa mkuu wake Kamishna Nurdin,

Kamishna alipitia yale maelezo mwisho akaguna,je unadhani nini kiliendelea?! Twende katika hatua inayofuta...


HATUA YA KUMI NA SITA


"Hii kesi na mashaka nayo embu kwanza niitie Insp Jonathan hapa..."


"Sawa afande!"


Fatma akatoka na kuelekea ilipo ofisi ya Jonathan...


Kwa upande wa Jona baada ya kumaliza maongezi na wale marafiki zake,ambapo walikubaliana jioni wakutane kivulini bar sambamba na inspekta Butu waongelee swala ilo Jona akawaruhusu Paul na Andrea wakaendelee na kazi!


Wakati wakiwa kwenye korido ndefu wakielekea mapokezi,njiani walikutana na Fatma ambaye yeye alikuwa akielekea ofisini kwa Jona.


"Afande Jona yupo ofisini kwake?!"


Wakati wakipishana Fatma akawapachika swali ambapo wote kwa pamoja walimwitika,Fatma akazidi kukaza mwendo kuifata ofisi ya Jona!


Afande Paul na mwenzake waliwasili mapokezi walisalimiana vizuri na yule mama na wanaye,wakaachana nao,kila mtu akachukua siti yake!,walijua tayari mama yule atakuwa tayari kashasikilizwa,


Jonathan na Fatma waliwasili ndani ya ofisi ya kamishna,wakapewa ishara waketi.


"Nimeitika wito afande,"


Kamishna sasa akanyanyua kichwa chake ambacho kilikuwa bize kuendelea kusoma yale maelezo katika lile kalabrasha lililoandikwa na Fatma!,


"Nimekuita kwa maana,nataka nikukabidhi zingatio lingine japo la awali ujalikamilisha,utajua jinsi ya kufatilia na vijana wako,pitia hili faili ripoti zote za uchunguzi utaniletea mimi,kwa sasa una mafaili mawili katika mkono wako kazi ipo juu yako"


Kamishna aliongea huku akimkabidhi Jona kalabrasha lile,Jona akalipokea na kuanza kulisoma!


Baada ya kulisoma na kulielewa si ndo akachukua picha aitazame sura ya huyo mtu alopotea.


Ile anaitazama akuamini alichokiona!,


Macho ya mshangao yakamtoka,sura ile aikuwa ngeni machoni mwake,aliikumbuka fika,akajikuta mikono ikimlegea na kushindwa kuishika vizuri ile picha,


Akaiachia!..


Mshangao aloupata ulimshangaza Nurdin na hata Fatma,kwa uzoefu wao wa kipolisi walijua tu kushtuka kwa inspekta yule kuna sababu!


"Vipi inspekta mbona umeshtuka au unamjua mtu huyo?!"


"ha..ha..hapana mkuu!"


Jona akajikuta akipatwa na kigugumizi kikali,kamishna akawaruhusu, wakanyanyuka na kila mmoja akatoa heshima kwa mkuu wao,wakageuka na kuufata mlango kalabrasha lile sasa likiwa mkononi kwa Jonathan,walifika mapokezi,Jona akampa pole yule mama.


"Usijali mama hakuna lolote litakalo wapata na nikuhakikishie tutawakamata wauaji kuwa na amani mama yangu"


Jona aliongea kwa majonzi,kama vile ajui kitu,palepale akamwomba Fatma pamoja na binti mwingine kruta waelekee nyumbani kwa yule mama wakawe walinzi kwa muda,walichukua namba za ile gari,baada ya kuondoka ndipo Jona alipowapa ile picha wenzake ambao nao walishtuka vilevile,wote wakasoma kalabrasha lile na kulielewa vizuri!..


Kumbe huyu jamaa alikuwa ni mfanyakazi wa ofisi ya Raisi!,ila hawakuwa na shaka kuwa pia alikuwa ni muuzaji wa madawa ya kulevya!


Ilikuwa lazima wamjulishe inspekta Butu juu ya jambo lile haraka iwezekanavyo,hawakutaka kusubiri tena usiku kukutana Kivulini Bar.


Inspekta Jona akashika simu yake na kutafuta namba za Butu akazipiga,simu ikaita punde ikapokelewa.....


***


Butu furaha ilienda mbali na yeye,majonzi yalimtawala,alizidi kugida bia kwa uchungu,katu akujua kila anachofanya mwanaume wa kazi Zidu kite alikuwa akifatilia katika simu yake alounganisha na camera ndani ya nyumba ile!


Nje ya nyumba yake,mita kadhaa usawa wa barabara,ni muda mrefu alionekana binti mmoja kichaa pembeni ya mtaro akiwa na pochi lake chafu


Macho ya kichaa yule yalikuwa eneo la geti ilipo nyumba ya Butu!


Pia mtaa wa pili kutoka mtaa ule katika moja ya restraunt ilipaki pikipiki

ambayo ilikuwa ikimilikiwa na kijana mmoja alokuwa ndani ya gwanda za jeshi macho yake yalikuwa bize na tv ilokwepo pale.


Ni toka asbuh mjeda yule alikwepo pale.


Na siyo siku hiyo tu,


Hapana!!!....


Alishamaliza wiki alikuwa akija asubuh na kukaa pale mchana alikula pale usiku alikula pale saa tatu ndipo alipo ondoka


Butu pale sebuleni aliendelea kugida bia ghafla akapata wazo,muda ule ule mwanaume akajinyanyua na kufungua mlango,akatoka mpaka nje na kuchukua pikipiki yake,akaiwasha alipofikia getini akashuka akafungua geti na kutoka,ile katoka tu,yule kichaa akaingia ndani ya mtaro akawasiliana na yule mwanajeshi ambaye mara kibao kwa siri sana alikuwa akimfatilia Butu.


Baada ya mjeda yule kutaharifiwa alitoa simu yake na kumpigia Zidu.


"Mtu wetu katoka bad garl kanambia sijui anaelekea wapi ila ndo namfatilia"


"Nami nakuja akikaa position nzur mwangamize tu amri ishatoka"


Zidu kule nyumbani alinyanyuka naye akapakia tukutuku lake akatoka,silaha kibindoni!,alizidi kuwasiliana na yule mjeda kupitia vinasa sauti kutoka kwenye simu 'earfone' zilizopo masikioni mwake!


Butu alizidi kukanyaga mafuta pasina kuwa na shaka na mwanajeshi alokuwa akimfata nyuma akiwa juu ya pikipiki,


Mwanajeshi yule hakuwa mwingine zaidi ya Isack


"Ukifika usawa wake hakikisha kwa siri sana unammiminia risasi na kutoweka fastar hakikisha uachi ushahidi utakaowezesha kukamatwa kwako!"


Zidu akampa taharifa Isack ambapo alizidisha kasi ya pikipiki yake mpaka akamfikia butu akamuovar take sasa wakawa katika usawa,Isack sasa akaachia mkono mmoja na kuupeleka kibindoni akaanza kuhesabu moja.. mbili..tat..


Akiwa na nia akikamilishe 'u' achomoe pistol na kumaliza kazi palepale!....


*HATARI*


KIZAAZAA....

ITAENDELEA

BLOG