Search This Blog

Saturday, February 26, 2022

FATE OF LOVE - 4

   

Simulizi : Fate Of Love

Sehemu Ya Nne (4)



Alitenga chakula na tukaanza kula huku tukiwa tunaangalia TV. Wakati tunaendelea tulisikia mtu anagonga hodi na ilibidi Vanessa akamfungulie. Nikamuona Naima akiwa anaingia na moyo wangu ulinipasuka sana kwani hatukuonana tena tangu ile siku tuliyonaniliu kule Tabata.....



ENDELEA..

Aliingia mpaka sebuleni nilipokua nimekaa akiwa ameongozana na Vanessa.

Vipi shoga, umenisusa.

Weacha tu shoga yangu yani nipo busy balaa. Nina madeni Vikoba basi yananichanganya akili.

Mmhh! shoga na wewe hujaacha tu.

Nikiacha si nitakufa shoga, bila Vikoba nitaishi vipi mimi hapa mjini.

Waliongea maongezi yao huku mimi nikiwa kimya nakata matonge ya ugali tu.

Shemeji yangu vipi mzima?

Naima alinisalimia huku akionyesha kuwa amechangamka sana.

Mimi mzima sijui wewe shem.

Niko poa kama unavyoniona.

Sawa karibu tule ugali.

Na nilivyokua na njaa, shoga hebu na mimi kaniletee sahani nikate ugali wangu.

Alimwambia rafiki yake Vanessa. Tukawa tunakula huku tukiendelea na story. Niliwaangalia jinsi Vanessa na Naima wanavyocheka na nikajiona mjinga sana kufanya mapenzi na Naima na wakati najua wazi kabisa kuwa ni rafiki wa mchumba wangu. Kitu kibaya zaidi ni kuwa nilifanya nae mapenzi hadi kinyume na maumbile kitu ambacho sijawahi na wala sikufikiria kama nitakuja kukifanya. Nilizilaumu sana pombe kwani kwa kiasi kikubwa ndo zilizochangia maana nilikua sijielewi kabisa.

Mtoto yuko wapi?

Amelala muda mrefu sana.

Mmhh! huyu mchumba wangu nae kwa kulala, muda wote yeye usingizi tu.

Halafu shoga nasikia ulihama kule Kigogo.

Ndio shoga, nimechoka mwenzangu kukaa uswahilini. Nilivyochukua hela zangu tu Vikoba nikaenda kulipa chumba Kinondoni, na sasa hivi ndo naishi huko.

Afadhali shoga yangu maana kule napo kulizidi uswahili.

Walikua wanaongea story zao ambazo hata nilikua sizielewi na baada ya kumaliza kula tu nikawaaga kuwa naingia chumbani kupumzika.

Aiii shemeji na wewe nimekuja kuwaona wewe unaenda kulala.

Muache bwana baby wangu leo hayupo sawa, si unaona mapema hii yupo nyumbani?

Vanessa alinitetea kwa rafiki yake

Anaumwa nini?

Anajihisi homa hivyo baadae hapa tunaenda hospitali.

Okay! pole sana shemeji yangu utapona.

Sawa shem asante sana.

Muda wote nilikua naongea lakini simuangalii usoni Naima kwani nilikua naona aibu sana. Nikaingia chumbani na kuanza kuutafuta usingizi.


**************** ****************


Siku ya safari ya kwenda China iliwadia ambapo David pamoja na mke wake Janeth walinisindikiza mpaka Airport. Niliagana nao na wakanitakia safari njema na mafanikio huko niendapo na nikawashukuru sana. Kwa mara ya kwanza kwenye maisha yangu niliingia kwenye ndege ya shirika la ndege la Emirates na saa 8 mchana ndege ilianza safari na kuiacha ardhi ya Kipawa. Nilipokua nikichungulia nje nilikua naogopa sana kwa jinsi palivyokua mbali na sisi tupo juu kiasi kile. Hali ya hewa ilikua nzuri sana hivyo safari ilikua tulivu kabisa na baadhi ya abiria wengine walikua wamesinzia. Baada ya masaa kama manne na nusu hivi tulifika Oman ambapo ilitakiwa nibadilishe ndege na kupanda ndege inayoenda China. Kilichonishangaza ni kuwa njiani tulitumia muda wa masaa kama manne na nusu lakini nilipoangalia saa kwenye simu niliona ni saa 5 kasoro za usiku wakati Dar tuliondoka saa 8 mchana. Kwa wakati huo nilikua sijajua vizuri kuhusu mambo ya time zone na jinsi masaa yanavyotofautiana baadhi ya nchi na nchi.Asikwambie mtu miji ya wenzetu imejengwa bwana maana ule uzuri niliouona wakati ndege inakaribia ardhi ya Oman sitakaa niusahau hata siku moja. Kitu kizuri ni kwamba kuna wahudumu wanaotoa maelekezo kwa wateja wote ambao wanabadilisha ndege hivyo na mimi nilielekezwa niende sehemu ambayo watu wanasubiri ndege ya kwenda Guangzhou, China. Kusema ukweli kwa mara ya kwanza niliona umuhimu wa kujifunza kiingereza maana kwa mtu mgeni na usafiri wa ndege kama mimi ningepata tabu sana maana wahudumu wote walikua wanaongea lugha nyingi ikiwemo Kiingereza. Baada ya masaa mawili tulipanda ndege na baada ya masaa kadhaa tulifika salama China na ilikua ni asubuhi kabisa jua linawaka. Nilivyoshuka nikamuuliza muhudumu mmoja sehemu ambayo naweza nikapata WI-FI ili niwasiliane na wenyeji wangu. Alinielekeza na baada ya kuunganisha niliona meseji zikiingia mfululizo kwenye WhatsApp ambapo niliona na jina laLucas, mwenyeji wangu anayenipokea. Alinielekeza kila kitu cha kufanya na kweli nilivyotoka niliona mtu akiwa ameshika bango lenye jina langu na niliitazama sura yake nikagundua kuwa ni yeye maana nilishaona picha zake kwenye simu.

Alex, karibu sana Guangzhou.

Asante sana kaka.

Vipi Tanzania wote wazima huko?

Wote wazima, David pamoja na mke wake wanakusalimia sana.

Nashukuru sana.

Akanipokea begi langu nililolibeba na tukaanza kutoka nje. Sio siri wenzetu wamepiga maendeleo sana kwani ile Airport ilikua ni kubwa kupita maelezo. Ukitazama kwa nje kuna maghorofa mazuri na marefu sana. Tulitoka mpaka nje na kuingia kwenye gari ya Lucas na kuondoka hapo Airport.


*************** ***************


Nilikaa China takribani wiki tatu na nikafanikiwa kukusanya mizigo yote ambayo nilitakiwa nirudi nayo Tanzania kwa kusaidiwa na Lucas ambaye alikua anaishi na mke wake raia wa Uganda na wana watoto wawili. Tulitafuta meli ambayo inapita Tanzania na tulifanikiwa kuipata na tukaandikishiana mkataba kwa ajili ya kusafirisha mizigo yetu. Tukalipia na kontena moja kubwa maana mizigo ilikua ni mingi sana. Tulimaliza mambo yote na mimi nikaanza kujiandaa na safari ya kurudi Tanzania. Baasa ya mwezi mmoja na siku kadhaa nikapanda ndege na kuunganisha safari kama wakati nilivyokua naenda. Namshukuru Mungu nilifika salama Tanzania ambapo Vanessa alikuja kunipokea akiwa yupo na mtoto. Vanessa alifurahi sana na akanikumbatia kwa nguvu na kunipiga mabusu yasiyokua na idadi. Vee alikua hajui kuendesha gari hivyo ilitubidi tukodishe Tax ambayo ilitupeleka mpaka kwetu. Tuliingia ndani na kukuta akiwa amepapamba sana huku akiwa ameweka sticker nyingi sana zenye ujumbe wa kunikaribisha tena nyumbani. Sio siri ilinigusa sana moyoni na nilimsogelea Vanessa na kumpa busu mwanana la mdomoni. Pia aliniandalia vyakula mbalimbali na kunitengenezea juisi ya matunda ambayo ilikua tamu sana. Kusema ukweli Vanessa alikua anajua sana kumlea mwanaume kwani alikua ananifanyia vitu ambavyo vilinifurahisha sana. Siku hiyo tulipeana raha sana usiku kucha kwani ule mwezi mmoja niliokaa China bila kukutana na mwanamke ulinifanya niwe na hamu sana. Hata sikumbuki tulirudia mara ngapi ila nilimpa Vanessa dozi nzito sana na wote tukakata kiu yetu na kupumzika.


Siku tatu baada ya kurudi nilienda nyumbani kwa David kuwasalimia maana ilikua ni kipindi cha likizo na watu wote wapo nyumbani. Waliponiona walifurahi sana haswa Winnie na Patrick ambao ndio tulikua hatujaonana siku nyingi sana. Niliwabebea na zawadi maana niliwajua kuwa wanapenda sana haswa Patrick.

Alex China imekufanya uzidi kupendeza.

Aliongea Happy kwa utani.

Kule tena, si unawajua kenge na nyoka walivyokua na mafuta mengi?

Haaa! Alex usiniambie kuwa umekula nyama ya nyoka.

Nakutania bwana, si ningebabuka mwili mzima.

Niliongea huku nikiwa nacheka sana. Mimi na Happy tukikaa pamoja muda wote ni kucheka tu maana wote tulikua tunapenda utani.

Kaka Alex mtoto wako amekua mkubwa eeh?

Winnie nae akaniuliza.

Ndio, sasa hivi anakaribia miezi minne.

Anaitwa nani?

Kelvin.

Wow! hongera sana.

Asante sana Winnie.

Tuliongea mambo mengi sana tukiwa tumekaa nje kwenye bustani hadi mida ya chakula ilipofika. David na Janeth walikua bado hawajarudi kwenye mizunguko yao hivyo nilipanga niwasubiri mpaka watakaporudi. Tuliingia ndani na wote tukajumuika kula pamoja. Tulikula huku tukiendelea na maongezi ambapo hapo ulikua ni utani tu pamoja na vicheko vingi. Baada ya kumaliza wote tukahamia kwenye TV ambapo Happy aliweka movie moja nzuri sana ya ngumi. Tuliangalia na kuifurahia sana mpaka ikaisha kisha akaweka nyengine inayofanana na ile ile. Wakati imefikia katikati niliinuka na kuelekea chooni maana haja ndogo ilikua imenibana.


Nilijisaidia na kumaliza na wakati natoka nikakutana na Winnie akiwa ananisubiri. Nilibaki nimesimama tu namshangaa na mara nikaona ananivamia mdomoni na kutaka tubadilishane mate. Kweli nikampokea na kuanza kubadilishana nae, na mara ghafla tukasikia mtu akiwa pembeni yetu. Tulivyogeuka alikua ni Happy na nilihisi kama miguu inanyong'onyea na kutumbukia ardhini...........





Alex! Winnie! Yani nilijua tu!!

Happy aliongea kwa sauti kubwa sana hadi nikaanza kuogopa. Akanisogelea na kunikamata shati langu kwa nguvu na kidume nikawa mpole.

Alex, unafanya nini Alex, unafanya nini Alex! Ina maana unatuchanganya mimi na ndugu yangu!! Alex kweli? Kweli Alex!!?

Muda huo Winnie alikua amejibanza pembeni kimya na nilimuona wazi akiwa anatetemeka.

Kumbe wewe ni mnyama kiasi hiko na umekosa aibu, hivi kweli unanichanganya mimi na mdogo wangu!? Alex!!

Happy alikua mkali mithili ya Mbogo na alikua anaongea kwa sauti sana hadi machozi yakawa yanamtoka. Mara akaniacha na kuhamia kwa mdogo wake ambapo alimzaba vibao mfululizo.

Na wewe malaya wa kike kuhangaika na watoto wenzio umeona haitoshi umeamua kuja kwa watu wazima. Kwanini una tamaa sana wewe?

Nisamehe dada nimekosa sirudii tena!

Aliongea Winnie huku nae akiwa analia.

Alex kukuamini kote kule na kukuthamini leo unakuja kufanya upuuzi kama huu, kweli Alex!?

Nisamehe Happy ni shetani tu amenipitia.

Kelele! tena nisikusikie unaongea upuuzi wa aina yoyote ile.

Mara Patrick akaja na kutukuta tukiwa kwenye ile hali.

Dada kuna nini?

Alimuuliza dada yake Happy ambaye alimuona akiwa na machozi usoni.

Hamna kitu mdogo wangu wewe rudi sebuleni tunakuja sasa hivi.

Patrick alionyesha kutoridhishwa na hilo jibu kwani alipomtazama na Winnie pia alimuona akiwa na machozi. Aliondoka huku akiwa anageuka geuka nyuma.

Alex, i hate you! ( Alex, nakuchukia ) na kuanzia leo naomba usiniongeleshe tena.

Aah aah! sasa hapo Happy unakua unakosea hebu punguza hasira tuyamalize haya.

Umalize kitu gani? Ina maana unataka kunifanya mimi kipofu au mtoto mdogo sijayaona haya? Sina kitu chochote cha kuongea na wewe na hongera sana kwa kuuchezea mwili wangu kwa kipindi chote hiko.

Aliongea na kuanza kuondoka ambapo nilijaribu kumshika mkono lakini aliutoa kwa nguvu.

Niache usinishike.

Happy nakuomba upunguze hasira tafadhali na unisikilize.

Happy hakutaka kusimama na aliondoka eneo hilo.

Si unaona sasa mambo yako ya kupenda kujiachia madhara yake haya? Leo siri imefichuka.

Nilianza kumtupia lawama zote Winnie.

Lakini mimi nimekumiss ndo maana nimekufata mpaka huku angalau unipe japo busu tu.

Hata kama ungesubiri tuwe wenyewe tu. Ona sasa.

Naomba unisamehe Alex, nakupenda sana ndo maana nashindwa kabisa kujizuia.

Hebu kwa muda huu tuachane na hayo mambo. Kwanza mimi sikai tena hapa naondoka.

Usiondoke Alex naogopa dada atanipiga.

Hawezi kukupiga tena maana hata yeye anaogopa mambo yasiwe makubwa haya hadi wazazi wenu wakajua. Kitu kikubwa ni kutafuta wakati mzuri na kumuomba msamaha.

Sawa Alex nitafanya hivyo.


Nilianza kuondoka na nilivyofika sebuleni nikamkuta Happy akiwa yupo na Patrick na hakutaka hata kuniangalia.

Patrick bye mimi naondoka.

Aaah! kaka Alex kwani si ulisema unakaa mpaka baba na mama warudi.

Ndio mdogo wangu ila nimepigiwa simu ghafla kuna sehemu inabidi niende haraka.

Ilibidi nimdanganye Patrick ili aweze kunielewa.

Dah! sawa, utakuja lini tena?

Siku hizi hizi nitakuja tena na kukupeleka movie wala usijali mdogo wangu.

Niliongea huku nikijitahidi kutabasamu ili anione nipo sawa. Muda wote Happy alikua kimya na alionekana kuwa na hasira sana. Sikutaka tena kumuongelesha na nikapanga nimuache mpaka hasira zake zitakapopungua.

Yeeee! halafu twende na beach.

Patrick aliongea huku akionyesha kuwa amefurahi sana kumwambia vile.

Sawa usijali Patrick tutaenda na beach.

Alinielewa na nikatoka hadi nje ambapo niliingia kwenye gari na kuanza safari.


*************** ***************


Zilipita wiki mbili tangu lile tukio la nyumbani kwa David litokee na Happy alikua yupo kimya tu wakati sio kawaida yake. Kusema ukweli hata mimi mwenyewe nilijiona wazi kuwa nimekosea sana kuwachanganya ndugu wa tumbo moja na nikawa najishauri nifanye nini ili nimuombe msamaha Happy ambaye alionekana kuwa na hasira sana. Nikapanga kuwa nitatafute muda mzuri haswa atakaporudi hostel ili nikamuombe msamaha maana nikienda nyumbani kwao itakua nafanya kazi bure tu.


Nikajitahidi kuyaweka pembeni mambo ya Happy na Winfrida japokua akilini bado yalikua yananisumbua sana. Agness nae alikua bado anaitesa akili yangu kwani alionekana wazi kuwa hana tena mpango wa kuachana na mume wake na kurudiana na mimi japokua bado alionyesha kuwa ananipenda. Bado sikukata tamaa juu ya penzi lake na nilikua naamini kuwa siku yoyote nitafanikiwa kumrudisha mikononi mwangu na kutimiza ndoto yangu ya kufunga nae ndoa.

Namshukuru Mungu nyumba yangu ilikaribia kabisa kuisha na vilikua vimebaki vitu vidogo sana kiasi kwamba mtu mwenye haraka anaweza hata kuhamia na kuishi. Ile safari ya kwenda China iliniingizia hela nyingi sana na bado David aliniahidi pesa nyengine zaidi pindi mzigo utakapofika salama. Bado nilikua sijavuta umeme japokua wiring na kila kitu kinachohusiana kilikua kipo tayari. Nilipanga kila kitu kikikamilika mpaka fenicha mpya na vitu vyote vya ndani ndio nihamie kwani sikua na haraka sana. Pia nikapanga kwenda kumchukua mama kijijini na kuja kuishi nae japo kwa muda tu maana nilimuonea huruma muda mwingi kuwa peke yangu. Asikwambie mtu kama bado haujajenga unaweza usitembelewe na watu wako unaowaheshimu kama baba, mama na wengineo kwani niliona haipendezi kabisa kumleta mama pale nilipopanga na kuishi nae. Wiki nzima hiyo Agness alikaa akilini mwangu sana kiasi ambacho kwa mtu yeyote yule aliyenizoea ni rahisi kunigundua kuwa sina furaha.

Alex mbona siku hizi hauna furaha mume wangu, yani muda mwingi unaonekana ni kama mtu mwenye mawazo sana?

Alikua ni Vanessa akiniuliza wakati tulipokua tunakula chakula cha usiku.

Mbona mimi nipo sawa tu Vee, labda kazi ndo zinanichanganya sana kwani siku hizi mambo yanazidi kuwa mengi.

Mmhh! sasa mambo ya kazi ndo mpaka nyumbani?

Ndio, muda mwengine unajikuta mambo hayaendi sawa hivyo lazima uwe na mawazo.

Mmhh! kama ndo hivyo pole sana mume wangu. Jitahidi bwana mawazo ya kazi uyaache kazini na kufurahi na mimi pamoja na mtoto wetu Kelvin.

Sawa usijali honey nitajitahidi na asante sana.

Halafu Vee Jumamosi Mungu akipenda nitaenda Tanga kijijini mara moja kumuona mama maana aliniambia kuwa anaumwa umwa.

Ooh! jamani, anasumbuliwa na nini?

Homa homa tu za hapa na pale si unajua tena uzee?

Ndio. Pole sana mume wangu.

Asante sana mke wangu.

Sawa mimi nikutakie tu safari njema na umpe pole sana mkwe wangu na kumsalimia.

Sawa usijali zimefika.

Nilimdanganya tu lakini lengo langu lilikua ni kurudi tena kwa Aggy kwani bado sikukubaliana na matokeo.


Kusema ukweli masuala yanayohusu moyo tuuachie moyo wenyewe ndo wenye kujua kwani kwa mapenzi mazito anayonionyesha Vanessa, basi Agness ningeshamsahau siku nyingi na kumpotezea lakini ilishindikana kabisa. Siku ya kwanza niliyomuona Vanessa club next door nilimchukulia kama ni wanawake walewale tu wa kupita nao na maisha yaendelee lakini imekua tofauti kabisa. Kitu kikubwa kilichonifanya nishindwe kuweka kambi ya kudumu kwa Vanessa ni Agness tu kwani nilishindwa kabisa kumsahau na muda wote nilitamani arudi mikononi mwangu.


Kweli ilipofika Jumamosi jioni niliondoka na kuelekea Tanga ambapo nilifika usiku mishale ya saa nne na kufikia hoteli niliyofikia mara ya mwisho nilivyoenda. Nilipumzika na kesho yake mapema sana nikatoka na kuelekea Sahare anapoishi Agness..........



Nilifika na kupaki gari mahali pale pale ambapo nilipaki mara ya mwisho nilivyoenda. Nikawa najiuliza nifanye nini ili niweze kuonana na Shaffih maana nilijua wazi kuwa kama nikimtuma tena mtoto akamuite atakataa kuja kama akigundua ni mimi ndiye ninayemuita. Nikaamua kupiga namba ambayo Aggy alinipigia siku alipokua ananilaumu kwanini nilimfata mume wake na kumpiga mkwara. Kweli ile namba iliita sana lakini haikupokelewa. Nikaamua kupiga tena na baada ya kuita kidogo ikapokelewa na nikasikia sauti ya kiume.

Hallo.

Hallo, habari.

Nzuri tu, nani mwenzangu?

Naitwa Alex nilikua na shida na Agness.

Kumbe ni wewe, hivi unamtafuta nini mke wangu wewe jamaa?

Eeh eeh! mimi nina shida na Aggy kwani hii namba ni ya nani?

Yote hayo hayakuhusu na siwezi kukupa mke wangu uongee nae.

Brother usitake kuniona mimi mshari. Na leo nimekuja kistaarabu sana nataka kuongea tena na wewe.

Ina maana umenifata tena? Hivi unanitafuta nini ndugu yangu?

Nakuomba uje pale pale kwa siku ile tuongee.

Ujue unanitafutia matatizo sana wewe.

Mara nikasikia simu imekatwa huku Shaffih akionekana kuwa tayari ameshapaniki.


Nikabaki najiuliza nifanye nini tena maana lengo langu lilikua ni kukutana naye uso kwa uso ili niongee naye. Wakati naitazama simu na kujiuliza kama nimpigie tena nikaona mtu akitoka kwenye ile nyumba anayoishi Aggy na nilipomtazama vizuri nikamgundua kuwa ni Shaffih mume wake Agness. Nilibaki ndani ya gari na kumtazama tu anataka kufanya nini kwani niliamini kuwa ametoka nje kwa sababu yangu. Nikamuona anaenda sehemu ambayo walikaa vijana watatu wakiwa wanacheza bao na kuanza kuongea nao. Alikua anaongea huku akionyesha kidole mahali ilipo gari yangu na nikajua watakua wananiongelea mimi tu. Baada ya kama dakika moja nikaona wote wanainuka na kuanza kuja mahali ilipo gari yangu. Muda wote huo nilikua sijashusha vioo na niliendelea kubaki hivyo hivyo huku nikiwa nimejiandaa kwa lolote linaloenda kutokea. Walifika mpaka nilipo na nikasikia watu wakiwa wanaongea kwa jazba sana. Waliigonga gonga gari kwa mikono na ilibidi nishuke na kujiweka tayari kwa lolote linaloenda kutokea.

Wewe ndo unaifanya ndoa ya mshikaji wetu ikose amani kisa hiki kigari chako, sio?

Aliongea kijana mmoja kati ya wale watatu kwa jazba sana.

Hivi unanitafuta nini wewe jamaa? Si nilishakwambia uachane kabisa na kuja huku kumfuatilia mke wangu?

Aliongea Shaffih ambaye nae alikua na jazba sana.

Kwani mnamchelewesha nini huyu mshenzi? Si tumpige tu tumshikishe adabu?

Aliongea jamaa mwengine ambaye alionekana wazi kuwa anatumia mihadarati ya aina yoyote ile kwa muonekano wake tu.

Jamani mimi sijakuja hapa kiushari, nafikiri hata wewe Shaffih nilikwambia hivyo hivyo mara ya kwanza.

Yani unamfatilia mke wa mtu halafu unasema kuwa haujakuja kiushari?

Aliongea kijana mwengine kati ya wale watatu waliokuja na Shaffih.

Shaffih hebu nisikilize tena. Sitaki mtu yoyote aumie na wala sitaki damu ya mtu yoyote imwagike. Naomba uniambie nikupe kiasi gani ulichotumia kumuoa Agness ili uachane nae.

Hivi wewe jamaa una akili kweli? Yani niachane na mke wangu kwa ajili ya hivyo vipesa vyako?

Jamani mimi naona hana adabu huyu tunamchelewesha tu.

Kweli bwana kama waliambizana vile kwani wote wanne walinivamia na kuanza kunirushia ngumi mfululizo. Nilijitahidi kujibu mashambulizi ambapo ngumi zangu baadhi ziliwapata na kuwaingia vizuri. Nilijitahidi sana lakini kwa wingi wao nilishindwa kukabiliana nao kwani mwisho kabisa walinizidi nguvu na kunilaza chini huku nikihisi kutokwa na damu mdomoni.

Watu wengi sana walijaa ambapo nilisikia kelele nyingi sana.

Utaacha kumfuatilia mke wangu au hauachi?

Aliongea Shaffih kwa jazba huku akiwa amenikalia kwa juu.

Siachi labda uniue.

Jamani mnamsikia huyu alivyokua jeuri?

Mara nikasikia ngumi tatu zikiniingia barabara usoni. huku wale wengine wakiwa wananipiga mateke ya mbavu na miguuni. Nilipatwa na maumivu makali sana hadi nikaanza kupiga kelele. Wakati wanaendelea kunisulubu nikasikia sauti ya Agness ambaye ndo alionekana kuwa anafika eneo lile huku akiwa analia sana.

Shaffih mume wangu mnafanya nini lakini?

Aliongea huku akiwa anajitahidi kumtoa Shaffih juu yangu ili aniachie.

Shemeji muache amfundishe adabu, hana heshima huyu jamaa.

Aliongea jamaa mmoja kati ya wale watatu.

Hapana mtamuumiza jamani naomba mumuache.

Na wewe unamtetea huyu malaya wako sio eeh? Unataka kuondoka nae?

Shaffih aliongea kwa jazba na kumnasa Agness kofi moja zito la uso. Aisee kile kitendo kilinifanya nipate nguvu za ghafla kwani sikujua niliinuka vipi pale chini na kumvamia Shaffih na kumtupa chini ambapo nilimpiga ngumi nyingi sana za uso.

Alex muache utamuua!!

Aliongea Agness kwa sauti kubwa sana.

Wale wenzake na Shaffih walinivamia tena na kuanza kunipiga ngumi na mateke ilimradi nimuachie mwenzao lakini sikusikia hata kidogo kwani niliendelea kumpiga ngumi za usoni hadi damu nyingi zikawa zinamtoka. Mimi pia nilipasuka sana usoni kiasi kwamba nilihisi damu zikichuruzika hadi mdomoni.

Alex muache mwenzio utamuuaaa!!

Aliongea Aggy kwa sauti kubwa sana huku akiwa analia. Mara nikaona raia wengine wakinivuta na kunitoa ambapo Shaffih alikua yupo hoi pale chini. Nilimtazama Agness ambaye nae alikua akinitazama huku akiwa analia sana. Agness alishindwa kuendelea kukaa pale kwani nilimuona akitoka mbio na kukimbilia anapoishi huku akiwa analia kama mtoto mdogo.


Jamani mambo gani haya ya aibu mnayafanya, si watu wazima nyie?

Aliongea mzee mmoja aliyekua amevalia kofia ya "Asalaam Aleykum".

Wale rafiki zake Shaffih wakataka kunivamia tena lakini yule mzee pamoja na watu wengine waliwatuliza.

Kwani nini tatizo?

Yule mzee aliuliza.

Huyu ms*ng* anamuharibia mwenzie ndoa yake yani mke wake hana raha kwa sababu ya huyu.

Aliongea yule jamaa ambaye muonekano wake ulikua ni wa mvuta bangi kabisa.

Aah aah! hebu punguza jazba basi na kutukana na unieleweshe vizuri.

Mzee wangu hakuna hata mmoja anayeujua ukweli hapa kuhusu mimi na yule mwanamke. Yule ni mwanamke wangu kabisa na huyu jamaa ametumia udhaifu wa ugomvi wetu tu kumchukua.

Niliongea kwa sauti ya busara sana kwa yule mzee

Lakini wewe si hakua mkeo na huyu tayari kashamuoa?

Ndio mzee lakini bado wote tunapendana.

Sasa hapo unakua unakosea mwanangu hata dini haisemi hivyo. Yule mwanamke tayari ni mke wa mtu na wewe hauna haki nae tena hivyo inabidi ukae nae mbali, sijui unanielewa.

Nilikaa kimya kuashiria kuwa yale aliyoyaongea hayakuniingia akilini hata kidogo.

Nakuomba mwanangu ujiepushe na hayo matatizo na ukae mbali na yule mwanamke kwani huyu kijana ana haki ya kwenda kukushitaki popote pale.

Mzee wangu, mimi naomba niondoke tu maana sipo sawa hata kidogo.

Natumaini umenielewa lakini na hautorudi tena. Wewe mtoto hebu kamletee maji anawe ili aondoke zake.

Aliongea yule mzee ambaye alionekana kuwa na busara sana.

Shaffih na wenzake wakaanza kuondoka kuelekea kwao huku wakinitazama kwa hasira sana.

Wewe k*** wewe una bahati sana. Jaribu kutokea tena huku kama hatujakuchinja.

Aliongea yule kijana ambaye alionekana kuwa muhuni sana. Sikumjibu kitu kwani nilichukua maji niliyoletewa na kuanza kunawa. T- shirt nyeupe niliyovaa ilikua haitamaniki kwa kuchafuka pamoja na kujaa damu. Niliivua na kubaki na vesti tu kisha nikanawa vizuri ambapo ndo nikaanza kusikia vizuri maumivu sehemu nilizoumia. Nilipomaliza nilimrudishia yule mtoto jagi lake na kumshukuru sana kisha nikaenda kuingia kwenye gari. Watu wote waliokuja kushuhudia wakaanza kutawanyika na mimi nikaondoka huku nikiwa na mawazo sana.


************** **************


Baada ya mlolongo mrefu hospitali na kunikatalia kunipa huduma, hatimaye walikubali kwani mwanzo walitaka niende kwanza polisi nikapewe PF3 maana waliogopa wasije wakaingia matatizoni. Ilibidi nitoe kiasi cha pesa kuwahonga kwani niliona nikienda polisi mambo yataanza kuwa mengi na kutaka kujua kila kitu kilichotokea na kunipotezea muda. Nilifungwa bandeji sehemu zote zenye majeraha huku nikishonwa nyuzi nne sehemu ya paji la uso. Baada ya kumaliza kunipatia huduma zote kwenye hospitali hiyo ndogo ya mtu binafsi, niliondoka na kupitia duka la nguo ili ninunue nguo maana ile T-shirt niliiacha kule kule kwenye tukio na jeans ilikua haitamaniki. Nilivyomaliza nilienda hotelini nilipofikia ambapo nilioga na kubadilisha nguo kisha nikaagiza chakula cha mchana. Muda huo nikawa nawaza nitamueleza nini Vanessa juu ya yale majeraha niliyoyapata kwani niliondoka nikiwa mzima kabisa.


Baada ya kumaliza kila kitu mida ya alasiri nilianza safari huku kichwani nikiwa na mawazo mengi sana. Nilifika salama Dar es salaam mida ya saa 3 usiku ambapo nilienda moja kwa moja nyumbani. Nilivyofika nilipiga honi getini ili nifunguliwe huku moyo ukiwa unanidunda sana nitamwambia nini Vanessa...........




Vanessa alitoka na kunifungulia geti kisha nikaingiza gari na kulipaki. Nilishuka na aliponiona alihamaki sana.

Baby! what happened? ( Baby! nini kimetokea? )

Aliongea na kunifata karibu kabisa.

It's a long story baby! thank God i'm fine. ( ni story ndefu baby, mshukuru Mungu niko sawa)

Mume wangu unanitisha sana, umepatwa na nini?

Twende ndani nitakusimulia kila kitu.

Vee alienda kufunga geti kisha tukaongozana hadi ndani chumbani ambapo nilimkuta mtoto wetu Kelvin akiwa ameshalala.

What happened baby? ( Nini kimetokea baby?)

Bado Vanessa alionyesha kuwa na uchu na shauku ya kutaka kujua.

I got atacked by the people i don't know. (Nimeshambuliwa na watu nisiowafahamu.)

What? When and where? ( Nini? Lini na wapi?)

Vanessa alionyesha kushtuka sana.

Jana usiku wakati ndo nipo njiani naelekea kwa mama. Nilifika sehemu na kusimama kwani haja ndogo ilikuwa imenibana sana. Nilivyomaliza kujisaidia wakati narudi kwenye gari ndo nikaona vijana watano wakiwa mbele yangu ambapo walianza kunipiga sana na wengine wakaivamia gari na kuanza kuisachi. Walipomaliza wakaniacha na kutoka mbio ambapo sikuweza kuishika sura hata ya mmojawapo.

Jamani, pole sana mume wangu.

Aliongea huku akinishika usoni kwenye majeraha yangu.

Asante mke wangu.

Kwahiyo baada ya hapo ikawaje?

Nilijikokota na kurudi kwenye gari na kukuta wamechukua pesa zote ambazo nilizotoa benki wakati naondoka ili nikampelekee mama. Zilikua laki nne na nusu ila kwa bahati nzuri hawakunisachi kwani simu pamoja na wallet vilikua mifukoni.

Pole sana mume wangu.

Asante mke wangu nishapoa.

Sasa kwanini tulivyoongea asubuhi haukuniambia?

Niliogopa naweza nikakutisha sana na kukupandisha pressure ndo maana nikasubiri hadi nirudi.

Mhh! Sawa, pole sana mume wangu, vipi lakini unavyoendelea?

Sasa hivi sijambo japo bado majeraha yanauma.

Pole mume wangu usijali yatapona tu.

Sawa mke wangu nashukuru sana.

Nilijua kuupanga uwongo vizuri kwani Vee aliamini kwa asilimia mia moja.

Aliniandalia maji ya kuoga na kunipeleka mpaka chooni ambapo aliniogesha kama mtoto mdogo huku akiwa muangalifu sana ili yale majeraha asiyatie maji na kunitonesha. Tukajikuta tunapandishana midadi sana na kuanza kuchezeana. Tulivyorudi chumbani tukaanza kupeana raha na kuanza kujisahaulisha hasira zangu zote za jana yake. Nilimpa dozi nzito sana ambayo ndani yake ilichanganyikana na hasira pamoja na mawazo. Tulimaliza na kila mtu aliridhika kisha tukaenda sebuleni ambapo aliniandalia chakula cha usiku.


*************** ****************


Lile tukio lililotokea Tanga bado lilikua akilini mwangu kwani Shaffih na wenzake walinidhalilisha sana. Nilikaa nyumbani wiki nzima nikiwa nauguza majeraha ambapo niliwasiliana na David na kumdanganya kama nilivyomdanganya Vanessa na David aliweza kunielewa. Tulishauriana kutafuta msichana wa kazi ili asaidie kazi za ndani pamoja na kumlea mtoto wetu kwani Vanessa alitakiwa arudi kazini. Kweli baada ya siku kadhaa tulifanikiwa kumpata msichana mmoja anayeitwa Amina mara moja akaanza kazi. Vee hakupenda kabisa msichana wa kazi awepo ndani kwake ila hakua na jinsi tu. Nilimtaarifu rafiki yangu James juu ya kilichotokea wakati nilivyoenda kwa Agness na alikuja kuniona.


Sasa kwanini Alex unafanya hivyo ndugu yangu, si unajitafutia matatizo?

James nafikiri unajua ni jinsi gani ninavyompenda yule mwanamke.

Sawa lakini usitumie kigezo cha kumpenda ndo ukajiletea matatizo. Sasa hivi Agness ni mke wa mtu hivyo yule jamaa ana haki ya kukufanya chochote hata kukushitaki mahakamani.

Hapana James mimi kwa hilo nipo tayari kwa lolote hata kufa. Nampenda sana Aggy na sipo tayari kumuona anatumia muda wake wote na mwanaume mwengine tofauti na mimi.

Alex hebu jihurumie ndugu yangu, wahurumie na hawa watu waliokuwa nyuma yako. Tayari una mtoto sasa hivi anakutegemea. Kijijini kule mama anakutegemea na wewe ndo kama jicho lake lililobaki. Hivi kwanini Alex hauwazi yote hayo?

James nakuheshimu sana rafiki yangu ila kwa hili naomba uniache peke yangu maana sikuelewi hata kidogo. Hauwezi ukanishauri hata siku moja nimsahau Aggy wakati ndo mwanamke wa ndoto zangu hivyo naomba tuachane na hayo kabisa.

Sawa Alex ila nakuonea huruma sana rafiki yangu.

Sikumjibu kitu kwani niliona anaongea pumba tu.

Muda huo bado Vee alikua hajarudi kazini na Kelvin alikua anacheza cheza peke yake kwani alikua anakaa na sasa anajifunza kutambaa. Niliongea mambo mengine na James na ilipofika jioni aliniaga na nilimtoa nje kumsindikiza. Nikamuahidi kuwa nitakapopona nitaenda kumtembelea kwake anapoishi kwani nilikua sijafika hata mara moja.


Baada ya siku kadhaa nilienda hospital nyengine ya private kwa ajili ya kutolewa bandeji na nyuzi nilizoshonwa. Kwa sasa vidonda vilishaanza kupona na ilikua ngumu sana kwa mtu kunitambua kama nina majeraha mpaka anisogelee karibu kabisa.

Nikaamua kwenda kwa Happy kumuona pamoja na kumuomba msamaha kwa kile kilichotokea siku nilivyoenda kwao. Nilifika na kuingia mpaka ndani ambapo nilipofika mlangoni kwake niligonga hodi. Alikuja msichana mrembo sana ambaye sikumfahamu na kuanza kuongea nae.

Habari yako.

Nzuri karibu.

Asante. Samahani Happy nimemkuta?

Happy!!, samahani kwanza wewe ni nani?

Ni kaka yake naitwa Alex.

Alex! Hilo jina sio geni nahisi kama nilishawahi kumsikia Happy akilitaja. Hebu nisubiri hapo hapo nakuja.

Alirudi ndani na nikamsikia akiongea na mtu mule ndani kwa sauti ya chini sana. Baada ya kama dakika moja nikamuona Happy akitoka na kusimama mlangoni.

Alex umefuata nini huku?

Happy punguza hasira kidogo tusalimiane.

Salamu yako haiwezi kunisaidia kitu kwenye maisha yangu, naomba uniambie umefuata nini hapa?

Happy usinifanyie hivyo tafadhali naomba utambue mimi ni nani kwako.

Wewe ni nani? Si mfanyakazi wa baba tu.

Happy leo ndo unanijibu hivi kweli?

Ulitaka nikujibu vipi? Hivi ni binadamu gani wewe uliyekosa aibu kiasi hiko? Ina maana haujui kama Winnie ni mdogo wangu?

Happy punguza hasira basi tuongee na hiko ndo kitu kilichonileta hapa.

Uongee nini tena na mimi, una kitu gani cha kuniambia?

Happy umefika mbali sana mbona mimi na Winnie bado hatujafanya kitu chochote kibaya!

Weee! Tena naomba uishie hapo hapo usinifanye mtoto mdogo mimi ukanilaghai. Nimembana Winnie na ameniambia kila kitu kuwa tayari msha'sex tena sio mara moja.

Nilijikuta miguu yote inaishiwa nguvu kwani nilidhani Happy hajui kuhusu hilo.

Lakini Happy...

Lakini nini? bado haujaridhika unataka kunit** tena?

Sina maana hiyo Happy.

Kumbe una maana gani? Sikia Alex, naomba utakaponyanyua mguu wako hapa sasa hivi usikanyage tena eneo hili. Asante sana kwa kuuchezea mwili wangu na kunigombanisha na ndugu yangu.

Happy usinifanyie hivyo tafadhali kumbuka kuwa nakupenda.

Happy alicheka sana kisha akaendelea kuongea.

Unachekesha sana Alex, eti unanipenda. Na huyo mwanamke wako unayeishi nae? Na yule mwanamke wako wa kule kijijini? Unapenda wangapi? Hebu niache babu wee.

Kwahiyo Happy ndo unanifukuza kweli?

Ndio tena sitaki kukuona tena.

Nilinyongea sana na kuanza kuondoka taratibu huku mikono nikiwa nimeiweka nyuma. Nilitoka mpaka nje na kuingia kwenye gari kisha nikaondoka kurudi nyumbani.


*************** ***************


Ulipita takribani mwezi mmoja na nikawa najishauri niende tena Tanga tena safari hii niende kufanya ubaya nihakikishe kuwa nafanikiwa kumrudisha Agness kwenye himaya yangu. Kwa muda huo tayari majeraha yote yalishapona na nilikua nipo sawa kabisa. Nyumba yangu ya Mbezi ilishakamilika kila kitu na sasa mafundi walikua wanamalizia kujenga ukuta wa fensi tu. Pia kwa muda huo kodi yetu pale tulipopanga ilikua inaelekea mwishoni hivyo nikaona ni bora nikaingie kwangu tu kuliko kulipa tena kodi ambayo kwa miezi 6 ilikua ni karibia milioni 2 na nusu. Nikapanga pindi mafundi watakapomaliza kujenga fensi tu nihamie na fenicha mpya pamoja na vitu vyengine nitavinunua nikiwa nipo humo humo ndani.


Siku moja Janeth alinipigia simu na kunitaarifu kuwa niende hospitali kwani Winnie alikua amerudishwa kutoka shule akiwa anaumwa sana. Nilishtuka sana atakua amepatwa na kitu gani na ikabidi niache shughuli zangu zote na kuwahi huko.....



Niliendesha gari kwa haraka sana huku nikiwa na wasiwasi Winnie atakua amepatwa na tatizo gani. Nilifika hospitali moja maarufu iliyo Mikocheni na haraka nikashuka kwenye gari. Nilienda hadi mapokezi ambapo nilimkuta dada mmoja ambaye alionekana kuwa busy anaandika kitu.

Habari yako dada.

Nzuri, samahani nikuhudumie nini?

Nimekuja kumuona mgonjwa wangu anaitwa Winfrida David.

Okay! Pita korido hiyo hapo unayoiona hadi mbele kule utakuta mlango umeandikwa namba 14 ndo yupo humo.

Sawa dada asante sana.

Yule dada aliniitikia kivivu na nikajua ni kutokana na kuwa busy na kazi niliyomkuta anaifanya. Nilienda hadi mlango alionielekeza na nikafungua na kuingia ndani ambapo nilimkuta Janeth, Happy wakiwa pamoja na Winnie aliyekuwa anaumwa.

Vipi shemeji, Winnie amepatwa na nini tena?

Niliuliza huku nikionyesha kuwa na wasiwasi sana. Nikamtazama Happy ambaye mara ya mwisho tuliachana akiwa amekasirika sana na hataki hata kuniona wala kuongea na mimi. Nikaamua nimsalimie tu ili mama yake asihisi tofauti yoyote kati yetu.

Mambo vipi Happy?

Poa.

Vipi mzima?

Mzima.

Alinijibu kwa mkato tu huku akiwa hata hanitazami usoni.

Juzi jioni matron wake shule alinipigia simu na kunitaarifu kuwa Winnie hayupo sawa, joto limepanda na tumbo linamuuma sana. Tukashauriana kuwa wampeleke kwenye zahanati iliyo jirani ili akapatiwe matibabu lakini jana mchana walinitaarifu kuwa hali imezidi kuwa mbaya hivyo ndo imebidi tumrudishe huku na kumleta hospitali kubwa ili apatiwe matibabu zaidi.

Aisee poleni sana jamani. Kwahiyo kinachomsumbua sana ni tumbo na homa tu?

Ndio ana typhoid na Malaria wadudu watatu ila leo hii analalamika na kichwa pia kimeanza kumsumbua.

Mmhh! Sasa tatizo litakua nini?

Hamna kawaida tu. Ujue wanangu huwa hawaumwi mara kwa mara lakini pindi wanapokuja kuugua basi lazima uogope. Hata Happy wakati anasoma sekondari tulishawahi kumrudisha kama hivi tena alikuwa hoi zaidi ya hivi unavyomuona Winnie.

Muda huo Winnie alikua amesinzia tangu nilivyofika na nilimuacha tu apumzike pengine labda akiamka anaweza akawa na nafuu japo kiasi.

Kwahiyo hapa hospitali amefika muda gani?

Niliuliza huku bado nikiwa nimesimama tangu nilivyofika.

Tangu saa 12 asubuhi nipo hapa, Happy amekuja kama saa 3 hivi. Jana jioni sana ndo alianza safari kwa kutumia gari binafsi iliyokodiwa huko huko kwani tulituma hela ili awahishwe. Amefika Dar alfajiri kama saa 11 kwani tulimsihi dereva aendeshe taratibu sana.

Okay! Poleni sana. Vipi maendeleo yake kwa sasa tangu afike hapa?

Angalau nafuu naiona tofauti na wakati tunamleta asubuhi na baba yake. Hata tumbo amesema limeacha kukata na linauma kwa mbali sana.

Nilimuelewa Janeth kwa majibu yote aliyonipa na nikabaki namtazama Winnie tu. Muda wote huo Happy alikua yupo kimya tu na nikajua bado ana hasira na mimi.


Tulikaa sana na kupiga soga huku Happy akijilazimisha kuchangia neno moja moja ili mama yake asimshtukie kwa kukaa sana kimya wakati sio kawaida yake. Alikuja nesi na kutuambia kuwa muda wa kuona wagonjwa ulikua umeisha mpaka jioni na tuliweza kumuelewa. Tukatoka na tulimuacha nesi akiwa anajiandaa kumuwekea Winnie dripu ya tatu kati ya tano alizopangiwa.

Sasa Alex itabidi wewe uondoke na Happy ukamuache Mlimani City pale atachukua hata bajaj aende hostel maana mimi narudi nyumbani kuandaa chakula cha mgonjwa.

Nilishtuka sana kwani mimi na Happy kwa muda huo tulikua hatupo sawa hata kidogo. Nilimtazama Happy mwenyewe ambaye hakusema kitu chochote.

Sawa shem nimekuelewa, tutaonana jioni basi nitakuja tena.

Sawa Alex nashukuru sana.

Janeth aliongea na akaagana na Happy kisha akaingia kwenye gari yake na kuanza kuondoka. Happy ingia kwenye gari basi tuondoke.

Happy alinitazama usoni na kunipa msonyo huo sio wa kawaida.

Happy usinifanyie hivyo jamani hata kama nimekosa. Nimekuomba sana msamaha lakini bado moyo wako hautaki kurudi nyuma.

Don't talk to me. (Usiongee na mimi)

Aliongee kwa ukali kidogo huku akianza kuondoka.

Unaenda wapi sasa Happy?

Hakunijibu kitu na alizidi kutokomea. Sikua na jinsi kwani ilinibidi niingie kwenye gari na kuanza kuondoka. Nilivyofika nje nikamuona Happy akiingia kwenye bajaj. Roho iliniuma sana na kujikuta nazidi kujilaumu kwa ule ujinga nilioufanya hadi Happy akaninunia kiasi kile wakati tulikuwa tunaelewana sana. Nilirudi kwenye majukumu yangu ya kila siku kama kawaida huku kichwani bado nikiwa na mawazo sana juu ya mustakabali wa ugomvi kati yangu na Happy.


*************** ***************


Baada ya siku 4 Winnie aliruhusiwa kutoka hospitali na kurudishwa nyumbani kwao ambapo kwa sasa alikuwa na nafuu kubwa sana kiasi kwamba unaweza ukaongea nae na akafurahi kabisa. Nikamuahidi kuwa nitaenda kumtembelea nyumbani kwao pindi itakapofika wikiendi na alinishukuru sana kwa kuwa nae bega kwa bega kipindi chote wakati yupo hospitali kwani sikupitisha hata siku moja bila kwenda kumuona. Kwa Happy bado hali iliendelea vile vile kwani mara kadhaa nilizokutana nae hospitali alikua bado ana hasira na mimi na hakutaka kunitazama hata kidogo. Ilinibidi nianze kuyazoea yale maisha maana nilishajitahidi sana kumuomba msamaha lakini hakunielewa.


Namshukuru Mungu ujenzi wa nyumba yangu ulikamilika kwa asilimia 99% kwani vilibaki vitu vidogo vidogo sana vya ziada. Tukaamua tuhamie huko maana pale tulipokua tunakaa tayari kodi ilishafikia ukingoni na tulikua tunadaiwa kodi ya miezi mingine sita ambayo kama tungeendelea kukaa ingetulazimu tulipe. Niliongezea kununua vitu vyengine kama vitanda na magodoro maana ile nyumba ilikua ina vyumba vinne wakati sisi tulikua na kitanda kimoja tu.Tulinunua mahitaji yote ya muhimu na nyumba ilipendeza sana. Vanessa ndo alionyesha kufurahi kupita maelezo maana aliamini kuwa sasa tunaenda kuoana na yale ndo yangekua makazi yetu ya kudumu. Mtoto wetu Kelvin alikua amechangamka sana na kwa kipindi hiko alikua ameshafika takribani miezi 7. Mpaka kipindi hiko mama yangu mzazi alikua hajui kama nilikua ninaishi na mwanamke na tayari nishazaa naye mtoto mmoja. Mwanzo nilichukulia ni kitu cha kawaida tu ila kadri siku zilivyozidi kwenda nikaanza kuona umuhimu wa kumuweka wazi juu ya lile jambo maana lolote linaweza kutokea. Ila kikwazo kilikuja sehemu moja tu, kuhusu Agness kwani sikutaka mama ajue kama nina mwanamke ninaishi nae maana nilishamuahidi kuwa nitapigana kufa na kupona ili Aggy arudi mikononi mwangu.

Mwisho nikakata shauri na kuamua tu kuwapeleka Vanessa pamoja na mtoto wangu Kelvin mpaka nyumbani kwetu ili mama akawafahamu maana kipindi kile Vee alipoenda kwenye msiba wa baba, mama hakufanikiwa kumuona ingawa yeye Vee alimuona mama na alikua anamfahamu. Japo Vee alikaa nyumbani takribani siku tatu lakini mama hakumuona kwani muda wote mama alikua yupo chumbani kwake tu kama wanavyokaa vizuka.


Tulifika salama nyumbani na mama alitukaribisha kwa ukarimu sana huku akionyesha kuushangaa kidogo ule ugeni.

Vipi maendeleo yako mama?

Nashukuru baba naendelea vizuri tu japo miguu na kiuno vinanisumbua.

Pole mama ndo uzee huo lazima viungo visumbue.

Tuliongea mambo kadhaa ya kujuliana hali kisha nikaanza kuwatambulisha Vanessa na mwanangu Kelvin.

Mama kwanza naomba nikuombe radhi sana kwa kutokua muwazi kwako kwa kipindi chote hiki na nilifanya hivi kwa sababu ambazo hata wewe naamini unaweza ukazielewa.

Kutokua muwazi kwa kitu gani mwanangu?

Huyu mtoto unayemuona ni mtoto wangu anaitwa Kelvin.

Wee, mtoto huyu amezaliwa lini na mama yake ni nani?

Anakaribia miezi saba sasa na huyu unayemuona hapa ndo mzazi mwenzangu.

Mama alimtazama Vanessa na Kelvin na alionyesha kushtushwa sana na ule utambulisho.

Jamani hebu mlete huyo mtoto nimuone.

Aliongea huku akionyesha kutoamini yale anayoyaona. Vanessa akampatia na mama akampakata Kelvin huku akiwa anamtazama sana.

Alex hii ni damu yako kweli yani umefanana nae sana. Hili paji la uso ni la marehemu baba yako kabisa yani. Sasa kwanini umenificha muda wote huo wakati nataka kuwaona wajukuu zangu?

Nisamehe sana mama ila nafikiri unaelewa kuhusu Agness na kila kitu kilichotokea. Kama ningemleta mapema nafikiri usingenielewa vizuri.

Mama alikaa kimya kuonyesha alirizika na jibu nililompa.

Mama karibu sana nyumbani, jisikie upo kwenu kabisa na nimefurahi sana kwa huu ujio wenu.

Alimwambia Vee ambaye alionekana kufurahi sana.

Asante sana mama hata mimi nimefurahi sana kukuona na kufika hapa nyumbani.

Kusema ukweli japokua Vanessa alikua ni msichana wa kisasa na anayeenda na wakati, lakini linapokuja suala la nidhamu na kujali huwa hayumbi hata kidogo. Alikua na adabu sana kiasi kwamba hata mimi nilifarijika. Tuliongea mambo mengi sana huku mama akiwa ananisihi nisimtelekeze mzazi mwenzangu kwani nitakua nimekosea sana na pia nitakua namuandalia mtoto wetu malezi mabovu. Niliweza kumuelewa japokua nilikua sijui nini kinaenda kutokea kwani akili na mawazo yote yalikua kwa Agness japo ameshaolewa. Pia nilimtaarifu mama juu ya kukamilisha ujenzi wa nyumba yangu na tayari tushahamia huko na mama alinipongeza sana kwa hatua niliyofikia na hakuacha kunisihi nizidi kuwa makini ili nipige hatua kubwa zaidi na nikamshukuru sana kwa baraka zake. Tulikula chakula cha usiku na wote tukaenda kupumzika ambapo Mimi na Vanessa tulilala vyumba tofauti kwani tuliona tukilala pamoja haitaleta picha nzuri kwa sababu bado hatujaoana.


**************** ****************


Siku ya tatu tulirudi Dar ambapo Vanessa alionyesha kufurahi sana na akaona sasa ameshajikatia tiketi ya kuolewa na mimi kwani tayari nilishampeleka kwa mama yangu. Alinishukuru sana kwa kumpenda na kumjali kiasi kile hadi nikafikia uamuzi wa kumpeleka nyumbani. Marafiki zake Aisha na Naima walikua wanakuja kutembea mara kwa mara na nilijitahidi sana kutokaa nao karibu kwani ile kumbukumbu ya kitendo nilichofanya na Naima bado ilikua kichwani kwangu. Sikutaka tena kile kitu kijirudie ndo maana nilikua najitahidi sana kumkwepa ili tusiwe karibu.


Wakati nipo chumbani na Vee yupo sebuleni nikaona Winnie akinipigia simu kwenye ile namba yake aliyokua anaitumia kwa siri sana. Nilipokea na kuanza kuongea nae ambapo alionekana kuwa amechangamka sana...........




Alex mambo.

Poa Winnie, mzima wewe?

Mimi mzima hofu kwako tu.

Niko poa kabisa. Mbona umechangamka kiasi hiko, uko wapi?

Nipo Ramada beach.

Wewe mtoto wewe kwa beach, umeenda na nani?

Nipo na marafiki zangu wawili.

Mhh haya bwana, vipi unaendeleaje na kuumwa?

Nishapona na ndo maana nimekuja huku.

Sawa, mimi nipo nyumbani hapa.

Unaweza kuja huku?

Hapana Winnie siwezi kutoka leo. Vanessa yupo halafu pia nimechoka sana.

Mmhh haya bwana. Nimekupigia nikwambie kuwa kesho kutwa narudi shule, kwahiyo..

Kwahiyo nini?

Aah Alex usijifanye mtoto mdogo bwana.

(Nikawa nishamuelewa anachokimaanisha)

Lakini si tulishakubaliana kuwa tusifanye tena Winnie?

Bwana Alex usinifanyie hivyo mwenzio nina hamu na wewe na hapa sirudi tena hadi mwezi wa kumi na moja nikimaliza form four.

(Wakati naendelea kuongea mara nikamuona Vanessa akiingia chumbani huku akionyesha kama anatafuta kitu)

Baby haujauona mkoba wangu?

Hapana sijauona, kwani uliuweka wapi?

Mhh hata sikumbuki.

Niliongea na Vanessa huku simu bado ikiwa sikioni.

Kwahiyo ndo hivyo nikishakamilisha kila kitu nitakutafuta ili tuongee biashara.

(Nilizuga kama naongea na mtu mambo ya kibiashara ili Vee asihisi kitu chochote.)

Mmhh wewe nawe huna lolote, ushamsikia huyo mwanamke wako huko unajifanya unazuga. Baadae ukipata muda nipigie.

(Aliongea Winnie hadi nikajihisi nataka kucheka)

Nikakata simu na kumtazama Vanessa aliyekua bado anatafuta mkoba wake.

Aanha kumbe niliuacha chumba cha huko tangu jana, yani nimejisahau kabisa.

Vee aliongea huku akiniangalia na kutabasamu na nikabaki natikisa kichwa tu. Nilicheza game tu kwenye simu huku nikimsikia Vee akiwa bado anapiga soga na marafiki zake sebuleni.


*************** ****************


Kesho yake nikaenda kukutana na Winnie kama tulivyopanga na tukaenda sehemu yetu ile ile tunayoenda siku zote. Kwa sasa angalau Winnie alikua amezidi kupata kimo na kutanuka hivyo yule muhudumu mpya tuliyemkuta hakutuletea zengwe la aina yoyote. Baada ya malipo na kujiandikisha majina yetu ya uongo ambayo huwa tunayatumia siku zote tunazoenda, alitukabidhi chumba na tukajifungia kwa ndani.

Ila Alex unazidi kunenepa na kuwa handsome inaelekea huyo wifi yangu anakupa mambo matamu sana.

Nilifurahi sana kisha nikamjibu.

Sio uongo, anajua kunipa mambo matamu ndo maana unaniona hivi.

Sisi tusio na ma'baby tutajiua mwaka huu.

Winnie aliongea kwa utani na kunifanya nicheke sana.

What do you like from me? (Unapenda nini kutoka kwangu) hadi uwe unanitafuta kiasi hiki na hauwazi mwanaume mwengine?

Nilimuuliza huku nikiwa namtazama usoni.

Everything about you, especially your d***. (Kila kitu kwako haswa mashine yako)

Mashine yangu ina nini?

Nilimuuliza huku nikianza kucheka.

Kubwa halafu tamu.

Winnie alinichekesha sana kwa majibu yake aliyonipa hadi nikawa namvuta mashavu yake.


Hatukutaka kupoteza muda kwani tulianza kuvuana nguo taratibu huku nikimpiga mabusu ya shingoni yaliyoanza kuamsha hisia zake. Nilimshika chuchu zake zilizosimama kama mnara wa Paris na kumuona akiwa anafumba macho kwa hisia. Nilipopeleka mdomo ndo akawa kama amepigwa na shoti ya umeme kwani nilimuona akishtuka na kutoa sauti tamu sana iliyopenya barabara kwenye ngoma za masikio yangu. Niliendelea kumnyonya chuchu huku mkono mmoja ukiwa unatalii kwenye pachu pachu hadi nikamuona akiwa anahema kwa shida.

Baby twende chooni kwanza.

Aliniambia kwa sauti laini sana na iliyojaa kila aina ya uvivu na kudeka.

Kweli nilimuinua na kuanza kuelekea chooni huku tukiwa tunanyonyana mate. Nikafungulia bomba la mvua na likawa linamwaga maji taratibu na kutulowanisha mwili mzima. Winnie alikua ananyoa kama dada yake Happy hivyo haikua na shida nywele zake zikiingia maji. Nikaanza kumpaka sabuni na kumsugua mwili mzima na nilipofika kwenye kipochi manyoya ndo nilipoyaamsha rasmi mashetani yake. Nilimsugua vizuri huku nikiwa nampiga mabusu mfululizo ya shingoni na mdomoni. Nilimsugua sana kisha nikafungulia maji vizuri na kumsafisha vizuri hadi akatakata. Mule mule chooni nikaanza kufanya vitu vyangu kwa kuzama kunako chumvini kutalii. Nilimchezeshea ulimi kwa muda mrefu sana hadi nikamuona anaanza kukosa nguvu za kusimama na kuanza kunielemea. Nikamuachia na yeye aanze kulitawala dimba ambapo kabla ya kitu chochote akaanza kuiosha dunguso na bila kuchelewa akaanza kutuma salamu. Sio siri damu changa zina raha ya aina yake ndo maana watu wengi wanakutwa na hatia ya kufanya mapenzi na wanafunzi maana wanakua hawaepukiki kirahisi haswa unapokutana na mtoto anayeyajua mambo kama Winnie. Pamoja na kumzidi Winnie takribani miaka nane au tisa, bado kwenye uwanja wa fundi seremala tulikuwa tunaenda sawa tu kwa sasa japo kwa kiasi fulani nilimzidi uzoefu. Aliitendea haki vilivyo dunguso yangu hadi nikaanza kuhisi miguu inatetemeka kwa utamu uliopitiliza. Nilipoona utamu unazidi kukolea na nakaribia kuandika goli la kuongoza nilimuinua na kumgeuza ashike ukuta kisha nikampeleka bwana mkubwa pangoni. Winnie alitoa sauti moja nzuri sana ambayo mpaka sasa nahisi kama vile ninaisikia hapa. Nilianza kumpelekea moto wa kufa mtu huku na yeye akiwa ananipa ushirikiano wa kutosha kwa kunipa mauno kuntu ya rojorojo hadi mtu mzima nikapagawa. Kwa raha nilizozipata sikuchukua hata dakika tano nikajikuta nishawaita wazungu kutoka ulaya waje kutalii kwenye pango la Winnie. Sio siri katika siku zote nilizokutana na Winnie ili siku nilipata raha za hali ya juu na nikajikuta namkumbatia kwa nguvu na kumpiga mabusu mfululizo mtoto wa boss wangu.

Wewe mtoto unajua kunipagawisha aisee yani unanifanya kama mtoto mdogo vile.

Winnie alibaki anacheka tu na kuifanya sura yake yenye ngozi nyeusi wastani izidi kupendeza.

Tulijisafisha kisha tukarudi chumbani ambako hatukuchukua muda mrefu mchezo ukaanza tena upya. Ile siku nilijikuta nikipiga nyayo tano za nguvu tena mfululizo hadi wote tukawa hoi.


*************** ***************


Mawazo ya kuwa na Agness bado yaliendelea kunitawala kwenye akili yangu na nikaona mume wake Shaffih ndo kikwazo kikubwa cha ndoto yangu kutokutimia. Nilifikiria vitu vingi sana vya kufanya na nikafikia uamuzi mgumu na wa kikatili maana nilishaona maneno na mkwara ulikua hautoshi kumfanya Shaffih aachane na Aggy.

Someone has to go, there's no another way. (Kuna mtu inabidi aende, hakuna njia nyengine)

Nilijisemea peke yangu huku nikikunja ngumi kwa hasira sana. Kiukweli nilijikuta naingiwa na roho ya kikatili sana ambayo hata sikujua imetokea wapi maana kwenye maisha yangu sikuwahi kufikiria hata mara moja kama kuna siku nitakuja kumwaga damu ya mtu. Ila kwenye suala la Agness niliapia liwalo na liwe ila ni lazima nimrudishe Aggy kwenye himaya yangu. Nikafikiria ni wapi ninaweza kupata bastola ili inirahisishie kazi na ilibidi nimtafute rafiki yangu Tariq ambaye alikua mjanja mjanja sana na nilikua nasikia habari zake kuwa anajuana na watu wengi sana wanaofanya matukio ya kuvamia na kuiba.


Tariq vipi mshikaji wangu.

Aah we jamaa wewe huna maana hata kidogo, yani tangu umpate yule mtoto mzuri basi ndugu zako umetutenga kabisa.

Hamna bwana sio hivyo mzee ila hapa kati nilikua na mambo mengi sana yameingiliana nafikiri pia ulisikia kama nilimpoteza baba yangu.

Ndio mzee nilisikia ila kipindi kile nilikua nipo Mwanza ndo maana nilishindwa kuja.

Usiwaze mzee. Sasa leo nimekutafuta nina jambo moja muhimu sana na nafikiri wewe peke yako ndo unaweza kunisaidia.

Jambo gani tena hilo mzee mbona unanitisha?

Nahitaji kupata paipu.

Paipu? Alex acha masihara bwana. Paipu wewe ya kazi gani?

Maisha ndugu yangu na sisi ni wanaume hivyo mambo ni mengi. Kiufupi ni kwamba kuna mtu inabidi awahi haraka iwezekanavyo.

Imekuaje tena maana hilo jambo ni kubwa ujue.

Mapenzi ndugu yangu. Mapenzi ndo yananifanya nifanye yote haya. Kuna mwanamke nampenda sana na kuna boya yupo nae. Nimeshamuonya sana aachane nae sasa anajifanya mbishi.

Alex ndugu yangu yani mwanamke tu ndo akufanye uchukue hayo maamuzi! Kwanza mbona yule demu wako ni mzuri sana sidhani hata kama huyo mwanamke unayemuhangaikia anamfikia.

Tatizo sio uzuri au labda mwanamke tu. Huyo ni zaidi ya mwanamke kwangu kwani tumetoka mbali sana na nina malengo nae. Hakika nimejitahidi sana ila siwezi kabisa kuishi bila yeye.

Dah! Sasa Alex unanipa mtihani sana, kama ingekua ishu ya hela hata mimi ningechangamkia haraka sana ila hii bwana.

Tafadhali Tariq nakuomba sana mshikaji wangu. Sina mtu mwengine tena ninayemtegemea kwa jambo hili ila wewe tu. Fanya juu chini ndugu yangu kuna hela nzuri tu nitakupatia.

Alex nafanya hivi kwa sababu wewe ni kama ndugu yangu na tumeshafanya mengi sana. Kesho jioni njoo nyumbani kwangu.

Asante sana Tariq, nashukuru sana yani hata sijui niseme nini.

Usijali mwanangu. Ila kuwa makini sana.

Sawa mzee usijali kabisa kuhusu hilo.

Tuliagana na nikarudi nyumbani maana nilikua ndo natoka kazini.


Kweli kesho yake nikaenda maeneo ya Magomeni anayoishi Tariq na ilibidi tukutane barabarani tu. Alipoiona gari yangu alikuja na kuingia ndani ambapo alivua begi mgongoni na kulifungua. Alitoa bastola ndogo na kunikabidhi ambapo nilihisi mikono yote ikitetemeka..............



Alex mashine ndo hii hapa, kuwa makini nayo sana.

Asante sana Tariq, ina risasi hii?

Ndio zipo 12 humo, kwanza unajua kuitumia vizuri?

Hapana ila kwenye kulenga tu haitonisumbua.

Sio kulenga tu kuna mambo mengine mengi.

Akaanza kunifundisha jinsi ya kuweka kwenye usalama pindi unapokua hauna matumizi nayo na jinsi ya kuiweka tayari wakati unataka kuitumia. Pia alinifundisha jinsi ya kuweka risasi na kuzitoa ambapo niliweza kumuelewa vizuri sana.

Jumatatu jioni nitairudisha naamini nitakua nishamaliza kazi yangu.

Sawa kuwa makini nayo sana hiyo maana huyo aliyenipa ni mafia sana.

Usijali Tariq sitokuangusha ndugu yangu.

Nilimkabidhi bahasha ambayo ndani yake ilikua na shilingi laki tano kama asante.

Ya nini hii.

Hii ni kama asante ndugu yangu.

Aah! yani wewe Alex wa kunifanyia mimi hivi kweli! Hebu acha masihara bwana.

Aliongea kwa mzaha huku akifungua mlango wa gari na kutoka nje.

Asante sana mwanangu, acha mimi niwahi basi.

Poa utanijulisha itakavyokua.

Poa usiwaze mzee.


Niliificha vizuri ile bastola chini ya kiti changu huku nikiwa nimeiweka kwenye usalama kama Tariq alivyonielekeza. Nilifika nyumbani ambapo nilikuta bado Vanessa hajarudi kutoka kazini kwake. Niliichukua ile bastola na kuingia nayo chumbani kwangu kisha nikaiweka kwenye begi langu dogo la mgongoni na kulificha katikati ya nguo zangu kabatini. Nilikaa chini na kushusha pumzi na kuanza kujiuliza kama kile ninachotaka kukifanya ni sahihi.

Hakuna namna inabidi aende tu, haiwezekani yule mjinga mmoja azuie ndoto yangu isikamilike. Aggy ni lazima atakua mikononi mwangu na nitamuoa tu.

Niliongea peke yangu huku nikiwa hata nguo sijabadilisha. Mfanyakazi akaja kunigongea mlango na kumleta mtoto wangu Kelvin ambaye aliponiona alifurahi sana na kuanza kucheka. Pamoja na umri wake mdogo aliokua nao, bado alikua ananitambua vizuri kwani kila aliponiona alikua anakuja mbio sana kwa kutambaa. Nilimpenda sana mtoto wangu kwani nilikua nahakikisha anapata kila kitu ambacho mtoto alistahili awe nacho. Nilicheza nae sana na kufurahi hadi Vanessa aliporudi kazini na wote tukaungana kufurahi na mtoto wetu.

Baby, keshokutwa Jumamosi naenda Tanga mara moja.

Kuna nini?

Kuna masuala ya kikazi naenda kuyafuatilia.

Mhh! Baby hiyo Tanga mbona siku hizi imezidi sana, si juzi juzi tu umetoka huko?

Sawa, kwani kazi ina mipaka? Kuna mambo muhimu sana naenda kuyafuatilia.

Twende wote basi.

Baby acha masihara bwana mimi siendi kustarehe huko naenda kwa ajili ya kazi.

Mhh! Naona wivu una wanawake wako wa zamani wengi huko.

Sasa kama wapo wanahusika nini na mambo yangu ya kazi. Hebu acha kuwaza vitu ambavyo havipo bwana mimi naenda kwa ajili ya kazi tu na narudi keshokutwa Jumapili.

Mhh! Haya.

Alinijibu kwa shingo upande huku akionyesha kutoridhika na ile safari yangu.


*************** **************


Kesho yake siku ya Jumamosi mchana wakati namalizia shughuli zangu Janeth alinipigia simu ili niende dukani kwake Kinondoni. Kweli nilimaliza kila kitu na kuelekea huko ambapo baada ya mwendo usiozidi dakika 25 nilifika.

Karibu sana Alex ngoja nimalizane na huyu mteja.

Sawa usijali endelea tu.

Nilimjibu huku nikikaa kwenye sofa lilikuwepo dukani hapo na kutoa simu yangu kuperuzi. Baada ya kama dakika tano yule mteja aliondoka na Janeth akanifata na kukaa pembeni yangu.

Mwenzangu jana bomu si ndo likataka kulipuka.

Eeh?

Ndio. David alinikaa kooni na kuniuliza maswali hayo ambayo mengine nilishindwa kumjibu.

Janeth hebu acha masihara, amekuuliza kuhusu nini?

Eti kama kuna mwanaume nipo nae maana hanielewi kabisa nyendo zangu na pia siku hizi nimepunguza kumsumbua kama nimezidiwa tofauti na zamani.

Mhh! Kwahiyo wewe ukamjibu vipi?

Nimemkatalia ila anaonyesha bado hajaridhika na majibu yangu.

Janeth usinitie matatizoni mimi mtoto wa watu na kusababisha nipigwe risasi ya kichwa.

Acha uwoga bwana kitu kama hiko hakiwezi kutokea.

Mhh! Mimi nawaogopa sana watu wapole huwa wanakua na hasira kali sana.

Usijali bwana hawezi kujua. Halafu yule mfanyakazi wangu Grace kama kuna vitu anavijua hivi sio bure.

Kwanini?

Muda sasa namuona simuelewi elewi tangu kipindi kile wewe upo pale nyumbani yani kama mtu anayejua kinachoendelea vile.

Mhh! Halafu hiko kitu hata mimi nakubaliana nacho maana hata mimi nilikua simuelewi kabisa. Sasa itakuaje?

Wiki hii hii anarudi kijijini kwao nitamuanzishia zengwe hilo hatoamini macho yake.

Fanya hivyo bwana asije akatoa siri ikawa shida.

Usijali hilo limekwisha.

Tuliongea mambo mengi sana huku akinigusia tukapeane mambo maana ni muda kidogo hatujakutana. Nilimuelewa ila nikamwambia hadi nitakaporudi maana nilikua na safari ya kwenda Tanga mara moja. Alinielewa na alifurahi sana kisha nikamuaga na kurudi nyumbani kujiandaa ili niondoke.


Siku hiyo ya Jumamosi Vee nae huwa anarudi kazini mapema sana hivyo nilimkuta akiwa amesharudi. Tulikula chakula cha mchana kisha Vanessa akanilazimisha sana tufanye mapenzi kwa kuhofia kuwa huko ninapoenda nitaenda kuchepuka. Sikuwa na mood hiyo ila nilijikuta namkubalia tu ili aridhike na mimi niondoke nikatimize jambo langu nililokusudia. Nilimpa nyayo mbili za haraka haraka na nikamuona akiwa ameridhika kabisa na kufurahi.

Kesho uwahi kurudi basi baby na uwe makini usipate matatizo kama siku ile.

Usijali baby safari hii nitakuwa makini sana na nakuahidi kuwa kesho nitarudi mapema sana.

Alinipiga mabusu mfululizo kisha nikaweka jeans moja, t-shirt na boxer kwenye kile kibegi kilichokua na bastola ambapo Vee hakuelewa kitu. Alinisindikiza mpaka nje na nikaingia kwenye gari kisha tukaagana na nikaondoka.


Nilifika Tanga mnamo saa 4 usiku na kwenda kwenye hotel yangu ile ile ambayo huwa nafikia siku zote. Hotel ile ilikua ndogo sana kiasi kwamba hata hawana vifaa vya kukagua mizigo ya mteja ili kugundua kama amebeba kitu cha hatari. Nilikaa kitandani na kuanza kutafakari ni mbinu gani niitumie ili nimpate Shaffih na kummaliza bila kuonekana na mtu yeyote. Niliitoa bastola kwenye begi na kuzitoa risasi kisha nikaanza kuifuta futa huku nikiwa nawaza ni kwa namna gani nitakavyovuta kiwambo na risasi zitakavyotua kwenye ubongo wa Shaffih na kummaliza. Kwa muda huo sikua tena na roho ya kibinadamu kwani roho ya kikatili ndio iliyonivaa na kutamani kuitoa roho ya Shaffih hata kwa muda huo. Niliwaza mambo mengi sana mwisho nikaamua kuirudisha bastola kwenye begi kisha nikaagiza chakula cha usiku. Nilikula na kumaliza kisha nikampigia simu Vanessa na kuongea nae kidogo kisha nikapumzika.


Kesho yake niliamka mapema na kuanza kufanya mazoezi madogo kama push-ups mule mule chumbani. Niliingia chooni na kujimwagia maji kisha nikatoka mgahawani kupata kifungua kinywa. Baada ya kumaliza nikatoka nje kutafuta wakala ili nisajili line mpya ya simu na hiyo yote ilikua ni katika mbinu za kuhakikisha nammaliza Shaffih. Nilifanikiwa kumpata wakala na nikasajili line kikamilifu kisha nikakodi bodaboda na kusogea mjini kidogo ambako nilinunua simu ndogo. Niliiweka ile line na kurudi hotelini kutafakari ni muda gani mzuri wa kufanya unyama ninaotaka kuufanya. Nikaona usiku ndo wakati mzuri kwani mchana ingekuwa rahisi sana kuonekana. Mipango yote niliyopanga ilikamilika na nikampigia simu Shaffih. Simu iliita na baada ya muda ikapokelewa na nikajitahidi kubadilisha kabisa sauti yangu ili asinigundue.

Hallo.

Hallo, habari yako.

Nzuri.

Naongea na Shaffih kama sikosei.

Kweli ndio mimi, wewe nani mwenzangu?

Naitwa Mbwana.

Mbwana wa wapi?

Wa hapa hapa Tanga naishi huku Donge.

Sawa ulikua na shida gani na namba yangu umeipataje?

Juzi nilikuja hapo mtaani kwako kukuulizia nikaambiwa haupo na nikaelekezwa kwako kwa mkeo ila nilikua na haraka kidogo nikashindwa kufika. Kuna jamaa yako nahisi mnafahamiana ndo alinipa namba yako.

Huyo mtu anaitwa nani?

Kusema ukweli sikumuuliza jina ila anaonnyesha mnafahamiana vizuri tu.

Sawa tuachane na hayo, shida yako nini?

Mimi bwana nataka nikupe tenda, si nimesikia wewe ni fundi seremala?

(Niliwahi kuwasikia rafiki zake Shaffih wakiongea siku ya kwanza kabisa niliyoenda kumuulizia Agness pale mtaani kwao.)

Ndio, ndo kazi yangu.

Sawa. Sasa nilikua nataka nikupe tenda unitengenezee madawati 50 kwa ajili ya shule yangu ya chekechea ninayotarajia kuifungua mwakani.

Madawati ya aina gani hayo?

Ndo maana nimekupigia simu ili leo usiku ufanye juu chini tukutane maana kesho asubuhi sana ninasafiri hivyo sitakua na muda.

Sawa hamna shida, kwahiyo tukutane wapi?

Nafikiri maeneo ya Donge huku itakua vizuri maana pia sio mbali na huko kwako.

Sawa boss nimekuelewa. Basi mida ya saa 2 hivi nitakujulisha wakati nakuja.

Sawa Shaffih nashukuru sana kwa ushirikiano wako.

Usijali boss nawe asante sana.


Tulimaliza kuongea na nikaona nimepiga hatua kubwa sana kuelekea kupata ushindi ninaoutarajia. Kuanzia muda huo nilihisi damu ikitembea kwa kasi sana huku vinyweleo vikinisimama kwa uoga na wasiwasi juu ya lile tukio zito ninalotaka kulifanya. Hadi muda huo sikuwa hata na fikra moja ya kughairi au kurudi nyuma niachane na huo mpango. Akili yangu ilishajiandaa kuitoa roho ya mtu na sikua na huruma hata kidogo kwa hilo na kadri muda ulivyozidi kwenda nilizidi kupata ujasiri. Mwili ulinichafuka sana kiasi kwamba nilipojaribu kula chakula cha mchana niliishia kutapika tu. Nafsi haikua tayari kupokea kitu chochote kwa muda huo kwani roho mbaya ndo iliyonitawala. Asikwambie mtu suala la kumtoa roho binadamu mwenzio ni zito sana kama bado hujazoea kwani ile siku nilishinda hovyo sana japo lengo langu lilikua ni kuua tu. Hata maji yalikua mazito kupita mdomoni yani hata sijui niielezee vipi hiyo hali.


Masaa yalizidi kusogea na hatimaye jua likazama kabisa na giza likachukua nafasi yake. Nilijiandaa kwa ajili ya mauaji na nikatoka kamili na kuanza kuelekea maeneo ya Donge ambako ndo nilipanga kukutana na Shaffih....




Vanessa alitoka na kunifungulia geti kisha nikaingiza gari na kulipaki. Nilishuka na aliponiona alihamaki sana.

Baby! what happened? ( Baby! nini kimetokea? )

Aliongea na kunifata karibu kabisa.

It's a long story baby! thank God i'm fine. ( ni story ndefu baby, mshukuru Mungu niko sawa)

Mume wangu unanitisha sana, umepatwa na nini?

Twende ndani nitakusimulia kila kitu.

Vee alienda kufunga geti kisha tukaongozana hadi ndani chumbani ambapo nilimkuta mtoto wetu Kelvin akiwa ameshalala.

What happened baby? ( Nini kimetokea baby?)

Bado Vanessa alionyesha kuwa na uchu na shauku ya kutaka kujua.

I got atacked by the people i don't know. (Nimeshambuliwa na watu nisiowafahamu.)

What? When and where? ( Nini? Lini na wapi?)

Vanessa alionyesha kushtuka sana.

Jana usiku wakati ndo nipo njiani naelekea kwa mama. Nilifika sehemu na kusimama kwani haja ndogo ilikuwa imenibana sana. Nilivyomaliza kujisaidia wakati narudi kwenye gari ndo nikaona vijana watano wakiwa mbele yangu ambapo walianza kunipiga sana na wengine wakaivamia gari na kuanza kuisachi. Walipomaliza wakaniacha na kutoka mbio ambapo sikuweza kuishika sura hata ya mmojawapo.

Jamani, pole sana mume wangu.

Aliongea huku akinishika usoni kwenye majeraha yangu.

Asante mke wangu.

Kwahiyo baada ya hapo ikawaje?

Nilijikokota na kurudi kwenye gari na kukuta wamechukua pesa zote ambazo nilizotoa benki wakati naondoka ili nikampelekee mama. Zilikua laki nne na nusu ila kwa bahati nzuri hawakunisachi kwani simu pamoja na wallet vilikua mifukoni.

Pole sana mume wangu.

Asante mke wangu nishapoa.

Sasa kwanini tulivyoongea asubuhi haukuniambia?

Niliogopa naweza nikakutisha sana na kukupandisha pressure ndo maana nikasubiri hadi nirudi.

Mhh! Sawa, pole sana mume wangu, vipi lakini unavyoendelea?

Sasa hivi sijambo japo bado majeraha yanauma.

Pole mume wangu usijali yatapona tu.

Sawa mke wangu nashukuru sana.

Nilijua kuupanga uwongo vizuri kwani Vee aliamini kwa asilimia mia moja.

Aliniandalia maji ya kuoga na kunipeleka mpaka chooni ambapo aliniogesha kama mtoto mdogo huku akiwa muangalifu sana ili yale majeraha asiyatie maji na kunitonesha. Tukajikuta tunapandishana midadi sana na kuanza kuchezeana. Tulivyorudi chumbani tukaanza kupeana raha na kuanza kujisahaulisha hasira zangu zote za jana yake. Nilimpa dozi nzito sana ambayo ndani yake ilichanganyikana na hasira pamoja na mawazo. Tulimaliza na kila mtu aliridhika kisha tukaenda sebuleni ambapo aliniandalia chakula cha usiku.


*************** ****************


Lile tukio lililotokea Tanga bado lilikua akilini mwangu kwani Shaffih na wenzake walinidhalilisha sana. Nilikaa nyumbani wiki nzima nikiwa nauguza majeraha ambapo niliwasiliana na David na kumdanganya kama nilivyomdanganya Vanessa na David aliweza kunielewa. Tulishauriana kutafuta msichana wa kazi ili asaidie kazi za ndani pamoja na kumlea mtoto wetu kwani Vanessa alitakiwa arudi kazini. Kweli baada ya siku kadhaa tulifanikiwa kumpata msichana mmoja anayeitwa Amina mara moja akaanza kazi. Vee hakupenda kabisa msichana wa kazi awepo ndani kwake ila hakua na jinsi tu. Nilimtaarifu rafiki yangu James juu ya kilichotokea wakati nilivyoenda kwa Agness na alikuja kuniona.


Sasa kwanini Alex unafanya hivyo ndugu yangu, si unajitafutia matatizo?

James nafikiri unajua ni jinsi gani ninavyompenda yule mwanamke.

Sawa lakini usitumie kigezo cha kumpenda ndo ukajiletea matatizo. Sasa hivi Agness ni mke wa mtu hivyo yule jamaa ana haki ya kukufanya chochote hata kukushitaki mahakamani.

Hapana James mimi kwa hilo nipo tayari kwa lolote hata kufa. Nampenda sana Aggy na sipo tayari kumuona anatumia muda wake wote na mwanaume mwengine tofauti na mimi.

Alex hebu jihurumie ndugu yangu, wahurumie na hawa watu waliokuwa nyuma yako. Tayari una mtoto sasa hivi anakutegemea. Kijijini kule mama anakutegemea na wewe ndo kama jicho lake lililobaki. Hivi kwanini Alex hauwazi yote hayo?

James nakuheshimu sana rafiki yangu ila kwa hili naomba uniache peke yangu maana sikuelewi hata kidogo. Hauwezi ukanishauri hata siku moja nimsahau Aggy wakati ndo mwanamke wa ndoto zangu hivyo naomba tuachane na hayo kabisa.

Sawa Alex ila nakuonea huruma sana rafiki yangu.

Sikumjibu kitu kwani niliona anaongea pumba tu.

Muda huo bado Vee alikua hajarudi kazini na Kelvin alikua anacheza cheza peke yake kwani alikua anakaa na sasa anajifunza kutambaa. Niliongea mambo mengine na James na ilipofika jioni aliniaga na nilimtoa nje kumsindikiza. Nikamuahidi kuwa nitakapopona nitaenda kumtembelea kwake anapoishi kwani nilikua sijafika hata mara moja.


Baada ya siku kadhaa nilienda hospital nyengine ya private kwa ajili ya kutolewa bandeji na nyuzi nilizoshonwa. Kwa sasa vidonda vilishaanza kupona na ilikua ngumu sana kwa mtu kunitambua kama nina majeraha mpaka anisogelee karibu kabisa.

Nikaamua kwenda kwa Happy kumuona pamoja na kumuomba msamaha kwa kile kilichotokea siku nilivyoenda kwao. Nilifika na kuingia mpaka ndani ambapo nilipofika mlangoni kwake niligonga hodi. Alikuja msichana mrembo sana ambaye sikumfahamu na kuanza kuongea nae.

Habari yako.

Nzuri karibu.

Asante. Samahani Happy nimemkuta?

Happy!!, samahani kwanza wewe ni nani?

Ni kaka yake naitwa Alex.

Alex! Hilo jina sio geni nahisi kama nilishawahi kumsikia Happy akilitaja. Hebu nisubiri hapo hapo nakuja.

Alirudi ndani na nikamsikia akiongea na mtu mule ndani kwa sauti ya chini sana. Baada ya kama dakika moja nikamuona Happy akitoka na kusimama mlangoni.

Alex umefuata nini huku?

Happy punguza hasira kidogo tusalimiane.

Salamu yako haiwezi kunisaidia kitu kwenye maisha yangu, naomba uniambie umefuata nini hapa?

Happy usinifanyie hivyo tafadhali naomba utambue mimi ni nani kwako.

Wewe ni nani? Si mfanyakazi wa baba tu.

Happy leo ndo unanijibu hivi kweli?

Ulitaka nikujibu vipi? Hivi ni binadamu gani wewe uliyekosa aibu kiasi hiko? Ina maana haujui kama Winnie ni mdogo wangu?

Happy punguza hasira basi tuongee na hiko ndo kitu kilichonileta hapa.

Uongee nini tena na mimi, una kitu gani cha kuniambia?

Happy umefika mbali sana mbona mimi na Winnie bado hatujafanya kitu chochote kibaya!

Weee! Tena naomba uishie hapo hapo usinifanye mtoto mdogo mimi ukanilaghai. Nimembana Winnie na ameniambia kila kitu kuwa tayari msha'sex tena sio mara moja.

Nilijikuta miguu yote inaishiwa nguvu kwani nilidhani Happy hajui kuhusu hilo.

Lakini Happy...

Lakini nini? bado haujaridhika unataka kunit** tena?

Sina maana hiyo Happy.

Kumbe una maana gani? Sikia Alex, naomba utakaponyanyua mguu wako hapa sasa hivi usikanyage tena eneo hili. Asante sana kwa kuuchezea mwili wangu na kunigombanisha na ndugu yangu.

Happy usinifanyie hivyo tafadhali kumbuka kuwa nakupenda.

Happy alicheka sana kisha akaendelea kuongea.

Unachekesha sana Alex, eti unanipenda. Na huyo mwanamke wako unayeishi nae? Na yule mwanamke wako wa kule kijijini? Unapenda wangapi? Hebu niache babu wee.

Kwahiyo Happy ndo unanifukuza kweli?

Ndio tena sitaki kukuona tena.

Nilinyongea sana na kuanza kuondoka taratibu huku mikono nikiwa nimeiweka nyuma. Nilitoka mpaka nje na kuingia kwenye gari kisha nikaondoka kurudi nyumbani.


*************** ***************


Ulipita takribani mwezi mmoja na nikawa najishauri niende tena Tanga tena safari hii niende kufanya ubaya nihakikishe kuwa nafanikiwa kumrudisha Agness kwenye himaya yangu. Kwa muda huo tayari majeraha yote yalishapona na nilikua nipo sawa kabisa. Nyumba yangu ya Mbezi ilishakamilika kila kitu na sasa mafundi walikua wanamalizia kujenga ukuta wa fensi tu. Pia kwa muda huo kodi yetu pale tulipopanga ilikua inaelekea mwishoni hivyo nikaona ni bora nikaingie kwangu tu kuliko kulipa tena kodi ambayo kwa miezi 6 ilikua ni karibia milioni 2 na nusu. Nikapanga pindi mafundi watakapomaliza kujenga fensi tu nihamie na fenicha mpya pamoja na vitu vyengine nitavinunua nikiwa nipo humo humo ndani.


Siku moja Janeth alinipigia simu na kunitaarifu kuwa niende hospitali kwani Winnie alikua amerudishwa kutoka shule akiwa anaumwa sana. Nilishtuka sana atakua amepatwa na kitu gani na ikabidi niache shughuli zangu zote na kuwahi huko...............



Kweli tulipangana vizuri na tukakubaliana kuwa kesho yake tu tuanze kula bata letu maana sasa paka ameondoka hivyo ni muda wetu panya kutawala.

Siku iliyofuata mapema sana nikaenda kwenye shughuli zangu za kila siku kama kawaida na ilipofika mida ya saa sita mchana Janeth alinipigia simu na kunitaarifu kuwa tukakutane kwenye hotel tuliyokua tunapenda kwenda iliyopo maeneo ya Kijitonyama. Kweli nilitangulia na kulipia chumba kabisa huku nikiwa namsubiri Janeth kwa hamu maana ni siku nyingi sana sijakutana nae. Baada ya kama nusu saa alifika na kunipigia simu ambapo nilimuelekeza chumba nilipo na baada ya muda mfupi aliwasili. Nilimfungulia mlango na akanivamia kwa kunikumbatia huku akinipiga mabusu mfululizo utadhani vile mtoto mdogo.

Alex nimekumiss sana yani huyo mwanamke wako anajua kunikomoa.

Nilicheka kidogo kisha nikamjibu.

Hamna sio sana bwana ila hata wewe upo busy sana ndo maana inakua ngumu kuonana.

Kweli, mambo mengi ukijumlisha na lile duka jipya Mlimani City linavyoumiza kichwa ndo usiseme.

Vipi kwani, kuna tatizo au?

Hamna ila oda zimekua nyingi sana halafu utakuta muda mwengine mzigo unakua umeisha dukani hadi uende stoo. Yani mtihani juu ya mtihani.

Kama ni hizo ndo vizuri matunda yanaonekana maana nilifikiri biashara inasuasua.

Tuliongea mambo mengi sana kuhusu biashara huku na yeye akiniuliza kuhusu marndeleo ya biashara ninazozisimamia.

Halafu Alex unazidi kupendeza ujue yani shavu linatoka hadi raha.

Janeth aliongea huku akinichezea mashavu.

Si nyie hapo ndo mnaninenepesha.

Sema mwanamke wako usitujumlishe wote bwana.

Aliongea kwa utani.

Sasa nyie wote si mnanipa mambo matamu, kwanini nisiwajumlishe wote sasa.

Hebu tuachane na yote nipe raha kwanza maana wewe mtoto mtamu kama asali.

Nilicheka sana kwa maneno ya Janeth na kweli sikumchelewesha kwani nilianza kumsogolea karibu na kumpiga mabusu ya uchokozi (smoochies) shingoni na mashavuni.

Alex bwana, usinipake shombo hebu nipe samaki mzima usinibanie.


Aliongea kwa sauti laini sana inayotokea puani.

Nikaanza kuipandisha blauzi yake juu taratibu na kukiona kifua chake kilichokua vizuri utadhani bado msichana mdogo na bado hajazaa watoto tena watatu. Niliitoa blauzi yote na kuanza kuishusha sketi yake fupi inayoishia magotini kwa juu kidogo huku ikiwa na mpasuo wa kichokozi. Muda huo bwana mkubwa dunguso alikua amekasirika balaa hadi suruali niliyoivaa ilikua imetuna. Janeth akaanza kunishika shika maeneo hayo ya dunguso ikiwa ipo ndani ya suruali na kunifanya nipate raha sana. Nilimvua sketi yote na kumuacha akiwa amebaki na kufuli na sidiria tu. Akaanza kunitazama kwa macho yake yaliyolegea na kuwa na mboni nyeusi sana. Nikajikuta ghafla namkumbuka Happy maana ukimtazama machoni mwake kwa karibu yani ni mama yake mtupu. Nikaanza kuvua shati nililovaa pamoja na vesti kisha nikamalizia na suruali. Nilibaki na boksa tu ambayo ilikua imeinuliwa juu na bwana mkubwa aliyekua na hasira za mbogo. Kama kawaida yetu tukitaka kupeana raha basi usafi kwanza kwani tuliingia chooni na kuanza kuogeshana huku tukichokozana. Baada ya wote kumaliza tulirudi chumbani ambapo kufika tu nikamuona Janeth akinisukumia kitandani na kuanza kuishika shika dunguso yangu iliyokasirika balaa. Akaanza kuninyonya shingoni kwa ulimi wake na kuhamia hadi masikioni ambapo nilihisi mwili kusisimka sana. Akahamia kifuani ambapo alianza kuninyonya chuchu zangu na kunifanya nipate raha za hali ya juu. Asikwambie mtu, katika sehemu ambazo sisi wanaume huwa tunazifurahia wakati wa tendo basi ni kunyonywa kwenye chuchu na wanawake zetu. Yani unaweza hata kutoa siri kama bibi yako ni mchawi bila kutegemea. Akaanza kushuka taratibu na kufika kwa bwana mkubwa ambapo alianza kutuma salamu kwa ustadi mkubwa sana huku akiwa anafanya kama anaking'ata ng'ata kichwa cha maiki. Muda wote huo kidume nilikua natoa sauti nzito ya miguno kuashiria yale mambo aliyokua ananifanyia yalikua yanapenya hadi kwenye medula oblongata na cerebellum. Sio siri Janeth alikua ni zaidi ya Nyakanga kwenye mapenzi kwani alijua haswa jinsi ya kunipagawisha hadi nikajikuta machozi mepesi yakichuruzika pembeni ya uso wangu. Alinipagawisha sana hadi nilipohisi nakaribia kuandika goli la kuongoza ndio nilipomzuia asiendelee. Ikawa zamu yangu kuanza kumpa raha ambapo nilianza kubadilishana nae mate kwaani nilimjua kuwa anapenda sana hiko kitu. Kweli nikaanza kumuona anaitika taratibu na nikahamia kifuani kwake na kuanza kuyanyonya matiti yake. Nilimnyonya sana huku nikiwa nazichezea chuchu zake kwa meno na kumsikia akitoa sauti kwa shida sana kulitaja jina langu. Kizaazaa kikaja nilipohamia kunako chumvini uvinza kufanya vitu vyangu kwani Janeth alizidi kupagawa na kunishika kichwani akisisitiza nisitoke kwani alikua anapata utamu wa hali ya juu. Nilimtembezea ulimi kwa muda mrefu sana hadi akawa ananitaka nianze kumpa dozi kwani tayari alishaiva tayari kwa kuliwa. Kweli baada ya kuona yupo tayari, sasa nikachukua dimba langu na kuanza kulitawala kama vile kiungo wa zamani wa klabu ya Barcelona, Xavi Hernandez. Nikaanza kupiga pasi fupi fupi kuwachosha wapinzani na kadri mchezo ulivyozidi kunoga ndo nilipoanza kupiga pasi ndefu za kuzaa magoli. Janeth alikua anajituma sana na kunipa ushirikiano wa kutosha kiasi kwamba alizidi kuniongezea mzuka wa kumpa dozi. Muda mwengine aliniweka chini na kuanza kunipa miuno ya rosti rojorojo utadhani tunacheza taekwando. Sio siri katika wanawake wote niliokutana nao kwenye maisha yangu, hakuna aliyemzidi utamu Janeth yani muda wote hakuchoshi. Baada ya safari ndefu ya kuvuka milima na mabonde, hatimaye wote tulifika salama Kigoma mwisho wa reli na tukabaki tumekumbatiana kwa hisia.

Asante sana Alex kwa hizi raha unazonipa. Hakika wewe ni mwanaume wa kweli.

Mimi pia Janeth, sio siri unanipa raha sana kuliko mwanamke yeyote yule niliyewahi kukutana nae kwenye maisha yangu.

Janeth alifurahi sana kwa sifa nilizommwagia na alinilalia kifuani huku akiwa anatabasamu.

Tulirudia tena mara mbili hadi wote tukarizika na tukaondoka hapo hotelini ambapo Janeth alielekea dukani kwake na mimi nikarudi kwenye shughuli zangu.


**************** ****************


Siku zile za David kuwa safarini tulizitumia kikamilifu kwani tulijiachia sana utazani sisi ndo mke na mume. Janeth akawa ananiita mpaka nyumbani kwake kwani sasa hivi yupo peke yake maana mfanyakazi wake wa ndani Grace alishamrudisha kwao kama alivyoniahidi maana alishamuhisi kuwa ameshtukia michezo yetu tunayoifanya. Muda wa kazi nikajikuta nautumia na Janeth kupeana raha tu. Tukatoka mpaka out kwenda beach kujiachia yani tulijisahau utafikiri mimi ndo mume wake.

Yani Alex kama isingekua David haki ya Mungu ningeolewa na wewe. Unajua kunipa raha.

Aliongea Janeth wakati tumekaa ufukweni huku tukipata vinywaji laini.

Ndo basi tena haijawa itabidi tuendelee kujiibia ibia hivi.


ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

BLOG