Search This Blog

Saturday, February 26, 2022

FATE OF LOVE - 5

   

Simulizi : Fate Of Love

Sehemu Ya Tano (5)


Hivi naona kama hatufaidi kabisa yani muda wote tunaishi kwa wasiwasi.

Ndo inabidi tusijiachie sana, hata hivi tunavyokuja beach tunakosea sana.

Sasa mimi nitafanyaje? Muda mwengine na mimi natamani kutolewa out na kudekezwa kama hivi sasa David yeye muda wote yupo busy tu hana hata huo muda wa kutoana out labda kwa mwaka mara moja.

Mhh! Hilo nalo tatizo, muda mwengine inabidi umkumbushe.

Hata ukimkumbusha yanaingia huku, yanatokea huku. Hajali hata kidogo. Ila ukimwambia una shida ya hela basi anakupatia muda huo huo. Sasa mimi shida yangu kubwa sio hela, nahitaji sana muda wake na aniridhishe kitandani.

Ina maana mpaka leo bado tu hali yake kitandani ndo vile vile?

We acha tu Alex, naona mume wangu ndo kashakua mbovu. Ndo yupo vile vile tena naona siku hizi ndo anazidi maana kupitisha miezi miwili bila kunigusa kwake ni kitu cha kawaida sana.

Daah! Pole sana.

Mmmm! Nishazoea, nitafanyaje sasa na kashakua wangu.

Tuliongea mambo mengi sana hadi jioni jua lilipozama. Nikamrudisha Janeth kwake kisha na mimi nikarudi kwangu.

Kufika nikamkuta Vanessa amenuna sana hadi nikaogopa na kuanza kujiuliza kuna tatizo gani tena.


Nilivyoingia chumbani nikaona mtu akinifuata nyuma huku akianza kulia na ilibidi nisimame na kumtazama alikua na tatizo gani

Alex, kumbe wewe ni malaya kiasi hiki!! Kwanini lakini umenifanyia hivi!!?

Aliongea huku akiwa analia sana na kunifanya nichanganyikiwe sana...........




Vee nini tena mbona ugomvi hauishi kila siku?

Niliuliza huku nikiwa na wasiwasi sana amegundua kitu gani.

Alex unatembea mpaka na rafiki yangu, kweli?

Aah aaah! rafiki yako yupi huyo mbona unapenda kunisingizia lakini?

Usijifanye haujui wakati ushahidi wote ninao. Umefanya nini na Naima?

Nilishtuka sana na nikajiuliza itakua ameambiwa na nani hiko kitu maana nilielewana na Naima kuwa ibaki siri kati yangu mimi na yeye tu.

Naima? Tumefanya nini?

Nikamuona anatoa simu yake na kuanza kunionyesha meseji mpaka picha nilizopiga na Naima ile siku niliyotoka nae out kwenda Tabata na kulala huko huko. Kumbe waligombana na Naima alimtumia meseji nyingi ambazo nilichati nae hivyo nikajikuta sina cha kujitetea maana ushahidi wote upo wazi.

Hivi haujaona sehemu zote za kufanya umalaya wako hadi utoke na rafiki yangu.!!?

Vanessa aliongea kwa uchungu sana akiwa analia huku akinipiga makofi yake dhaifu. Nilijitahidi kumzuia lakini hakunielewa hata kidogo na alilia sana.

Hivi unakosa nini kwangu Alex hadi hautulii? Ina maana kukupenda kote huku na kuwa mwaminifu kwako unaniona mjinga?

Vee hebu tulia basi mke wangu tuongee.

Sitaki. Unataka kuniambia nini nikuelewe?

Nimeteleza mke wangu halafu ni pombe tu ndo zilichangia ila haikua dhamira yangu.

Haikua dhamira yako kwa meseji hizi? Hivi ni upuuzi wa aina gani huu unaoufanya?

Naomba unisamehe mke wangu, nakiri kweli nimekukosea sana.

Alex unaniumiza sana, kwanini lakini?

Basi mke wangu naomba uniwie radhi nimekosa. Nilikua mjinga sana kufanya huo upuuzi na tangu hapo sijawasiliana nae tena kuonyesha kujuta kwa nilichokifanya.

Hapana Alex hili kubwa sana siwezi kukusamehe kirahisi kiasi hiki. Unamfanya yule malaya Naima leo ajitambe na kuniona mimi mjinga kunichukulia mume wangu. Mbona unanidhalilisha kiasi hiki?

Kidume nilibaki kimya na kuinama chini kwa aibu.

Alex naondoka siwezi kukaa hapa kwa sasa.

Unaondoka unaenda wapi sasa?

Naenda kwa shangazi yangu.

Tafadhali Vee naomba haya mambo usiyafanye kuwa makubwa sana hadi shangazi akajua. Nipe nafasi mke wangu nitarekebisha kila kitu na mambo yatakua sawa tu.

Hapana Alex siwezi kuendelea kukaa hapa kwa sasa, nahitaji kupumzika na kuwa peke yangu.

Vee, usinifanyie hivyo tafadhali naomba tukae chini tuyajenge mke wangu. Yule ni kahaba tu kama unavyosema na niliteleza sana kufanya huo ujinga ila wewe ndo mwanamke wangu ninayekupenda. Tafadhali naomba unipe nafasi nyengine nakuahidi kila kitu kitakua sawa.

No, not today, i have to go. (Hapana sio leo, inanibidi niondoke)


Nilishusha pumzi kwa nguvu na kumtazama Vanessa kwa unyonge sana.

Do you real have to go? (Unataka kweli kuondoka?)

Yes i want to. (Ndio, ninataka)

Sawa.

Nilimjibu kinyonge sana kisha nikatoka nje na kutafuta tax. niliipata na kurudi nayo kisha nikaingia ndani ambapo nilimkuta Vanessa akiwa anaweka baadhi ya nguo zake kwenye begi lake.

Tax ipo nje inakusubiri.

Vanessa hakunijibu kitu, alifunga zipu ya begi na kuwa tayari kwa safari. Nikaenda kumbeba mtoto wetu ambaye alikua yupo usingizini. Nikabeba na kibegi kingine kidogo kisha nikatangulia nje. Nilipatana bei na dereva hadi anapoenda Vanessa kisha nikamlipa na kuingiza begi ndani ya gari. Baada ya kama dakika tatu Vanessa alitoka akionyesha kuwa mnyonge sana na hakutaka hata kuniangalia usoni.

Aliingiza begi kwenye gari kisha nikamkabidhi mtoto ambapo na yeye aliingia kwenye gari na kukaa nyuma.

I'm sorry. (Samahani)

Nilimwambia huku nikimtazama kwa sura iliyojaa kila aina ya huruma. Vanessa hakujibu kitu na muda huo huo tax ikaanza kuondoka. Niliitazama hadi ikapotea na nikarudi ndani kinyonge sana. Muda huo mfanyakazi wa ndani alikua yupo chumbani kwake na sidhani kama hata alisikia ule ugomvi. Niliingia chumbani kwangu huku nikiwa na mawazo sana.


************** *************


Kwa mara ya kwanza kwenye maisha yangu nilianza kuuona umuhimu wa Vanessa kwani kwa siku mbili ambazo alikua ameondoka nyumbani, maisha kwa upande wangu yalikua tofauti kabisa. Nikirudi nyumbani nakua mpweke sana peke yangu na hata linapokuja suala la chakula huwa nayakumbuka sana mapishi yake kwani mfanyakazi alikua sio fundi sana kwenye mapishi na hakumfikia hata robo Vanessa. Niliboreka sana na nikawa nalala mapema sana tofauti na kila siku pindi Vanessa akiwa yupo.


Muda wote Janeth alikua anataka tuwe karibu tu na kupeana raha maana alinogewa sana na penzi langu utadhani sio mke wa mtu vile. Muda mwengine nilimkatalia na kujifanya niko busy ili kumuepuka maana niliona nikijisahau sana naweza nikajiletea matatizo.


Wakati nipo kwenye shughuli zangu mida ya mchana nilisikia simu yangu inaita na nilipoitoa niliona ni James ndiye anayenipigia. Sikusita, haraka haraka nikaipokea.

James, mambo vipi?

Poa Alex, inakuaje.

Poa ndugu yangu, wapi hiyo?

Nipo kijijini huku.

Umeenda lini?

Leo siku ya tatu hii nipo huku.

Sawa, vipi mazingira huko na raia wanasemaje?

Huku kila kitu fresh tu. Ila nimekupigia kuna kitu nataka nikwambie hata sijui kama unakijua.

Kitu gani hiko?

Jana nilikua natembea tembea nikakutana na yule Halima rafiki yake na Agness.

Eenhe!, ikawaje?

(Nikauliza kwa shauku maana nilijua zitakua ni habari zenye kumuhusu Agness tu)

Akaniambia kuwa mume wake Agness ameuliwa inasemekana na majambazi maana amepigwa risasi.

Aaaaahh! Acha masihara.

(Nilionyesha mshangao kana kwamba sijui kitu kinachoendelea.)

Ndio, wiki ya pili hii sasa.

Dah! kwahiyo imekuaje?

Ameniambia kuwa Agness amerudi yupo hapa kijijini na hali yake sio nzuri hata kidogo.

Anaumwa au?

Yani hata haieleweki, kama amechanganyikiwa hivi maana muda wote ni kulia tu. Ana mawazo sana yani.

Daah! Wewe umeenda kumuona?

Hapana sijaenda ila hapa nafikiria baadae niende.

Hebu fanya uende halafu utanipa ripoti kamili. Inabidi nifanye safari nije huko.

Itakua vizuri sana ndugu yangu. Sio vizuri kumuangalia tu Agness akiwa anapitia kipindi kigumu kama hiki peke yake.

Kweli kabisa James. Basi baadae utakapoenda utanijulisha.

Sawa usijali Alex tupo pamoja.

Asante sana James.


Alikata simu na nikabaki nimeduwaa kwa mawazo. Nikawa najiuliza kama Aggy hanifikirii vibaya juu ya mauaji ya mume wake maana kipindi cha mwisho cha uhai wake tulishagombana kama mara mbili hivi. Pia nikajiuliza kama nikienda kijijini naanzaje kwenda nyumbani kwa kina Aggy maana yeye mwenyewe na mama yake wote walikua hawataki hata kuniona. Nikajisemea liwalo na liwe ila ni lazima niende kijijini na nifanye lolote niwezalo ili nionane na Agness.


************** **************


Bado Vanessa alikua hayupo sawa na mimi kwani nikimpigia simu kumsalimia alikua anaongea kinyonge sana. Nilijitahidi kumuomba msamaha na kumbembeleza arudi nyumbani lakini hakuonyesha kuwa tayari kunisamehe. Alionyesha kuumia sana kwa kitendo nilichokifanya cha kutembea na rafiki yake wa karibu japo kwa sasa wamegombana. Alinitaka nimuache na nimpe muda kwani kwa wakati huo alihitaji kuwa peke yake ili ajisahaulishe kilichotokea. Niliweza kumuelewa japo kinyonge sana maana nilimmiss sana Vanessa ila niliogopa kwenda kumuona maana nilikua namjua vizuri shangazi yake jinsi alivyokua na mdomo na nilijua ataniwashia moto tu kwa nilichokifanya.


Ule upweke ulinitesa sana kwani ilipofika wikiendi nikaamua kwenda bar moja maarufu maeneo ya Sinza na kuanza kukata maji ili angalau nipunguze mawazo. Eneo hilo lilichangamka sana na wadada wazuri hawakuisha kujipitisha mbele yangu na kujishebedua ili niingie kwenye mtego. Kiukweli sikuenda eneo lile kwa ajili ya kukutana na mwanamke ila kadri pombe zilivyozidi kupanda kichwani nilijikuta nikianza kutamani kampani ya mtoto wa kike. Kweli nikaita dada mmoja mzuri sana ambaye kwa muonekano wake hakupaswa kabisa kuishi yale maisha aliyokua anaishi ya kuutumia mwili wake kama kitega uchumi. Alifanana na alikua na sifa nyingi za kuwa mke wa mtu na kutulia ila aliamua kuchagua maisha ya kudanga kama wasemavyo watoto wa mjini. Nilimuagizia mzinga wa wine na savanna kadhaa ambapo alikunywa sana hadi nikamuona anaanza kusinzia. Yule msichana alivutia sana na gauni lake alilovaa la kuacha mapaja wazi na kuyaonyesha maziwa yake lililonifanya nizidi kupandwa na hamu.

Hey unaishi wapi?

Naishi Kinondoni.

Tunaweza kuondoka muda huu maana nakuona unaanza kusinzia.

Kwangu au?

Hapana, sehemu yoyote nzuri kupumzika.

Sawa tuondoke.

Nikaona hapo tayari nishafanikiwa kuingia fainali ya kombe la dunia na ilibaki kucheza fainali yenyewe tu. Tuliondoka na kwenda kuchukua chumba hotel ambapo tulipeana raha usiku kucha. Kitu nilichokua makini nacho ni kutosahau kutumia zana pindi ninapokutana na wasichana wa aina hii kwani nilikua siwaamini hata kidogo. Yule msichana alikua mzuri na aliniburudisha sana kiasi kwamba muda huo nilijiona sina stress hata moja.


Kesho yake asubuhi na mapema baada ya kuachana na yule msichana na kumlipa hela yake nilirudi nyumbani kwangu. Nilivyofika tu baada ya kubadilisha nguo na kupanda kitandani kuendelea kuuchapa usingizi nilioukatisha hotelini, niliona simu yangu ikiwa inaita tena namba ikiwa ngeni. Nilishtuka sana kwani kwa jinsi nilivyokua mtu wa majanga, namba ngeni nilikua naziogopa sana. Niliamua kuiacha bila kuipokea na baada ya kukata muda huo huo niliona namba hiyo hiyo ikipiga tena.


Niliipokea huku nikiwa makini sana na mtulivu kusikilizia ni nani anayenipigia.

Alex, mimi Winnie.

Aanha Winnie, vipi mbona sauti yako ipo hivyo, una tatizo gani?

Alex nimeharibu sana, nimefukuzwa shule Alex.

Winnie alinijibu huku akiwa analia sana.............




ENDELEA..

Umefukuzwa shule? Hebu ngoja kwanza nyamaza ili unieleweshe vizuri.

Ndio nimefukuzwa shule.

Kwa sababu gani sasa?

Winnie hakujibu na aliendelea kulia sana hadi akaanza kunipa wasiwasi.

Winnie hebu nyamaza basi ili uniambie vizuri ujue unanichanganya sana.

Alex nina mimba.

Nini? una nini?

Winnie aliendelea kulia sana na kunifanya mtu mzima nizidi kupagawa maana nilijua ile mimba ni ya kwangu tu.

Winnie hebu acha masihara unasema una nini?

Nina mimba Alex.

Hiyo mimba ni ya nani?

Sasa unadhani itakua ya nani? Ni ya kwako.

Nilihisi hali ya kupooza, mfadhaiko na mbubujiko wa machozi ambao hata sijui ilitokea wapi.

Winnie hebu acha masihara bwana ujue nipo serious.

Utani wa nini sasa Alex wakati mimi nipo kwenye matatizo! Nina mimba yako na shule nimefukuzwa.

Wewe umejuaje kama una mimba?

Wiki ya pili sasa hii sijisikii vizuri yani muda wote najihisi kulala tu, kichefu chefu na kutapika hadi matron akaanza kunihisi vibaya. Juzi jioni ndo nikapelekwa hospitali na nikagundulika kuwa nina mimba ya wiki tatu sasa.

Winnie, imekuaje lakini mpaka ukashika mimba mbona unanitia matatizoni sana mimi?

Ile mara ya mwisho tulikutana nikiwa nakaribia siku zangu za hatari na kwa jinsi tulivyofanyana sana ndo maana mimba imeingia.

Dah! Winnie si unanipeleka jela mimi jamani kufungwa maisha? Vipi nyumbani wameshajua?

Ndio mama amepigiwa simu na anajua.

Wewe Winnie wewe.

Lakini bado hajajua kama wewe ndo muhusika nimegoma kabisa kumtajia.

Nakuomba Winnie unifichie hii aibu, hivi unafikiri nitaiweka wapi hii sura yangu?

Sawa ila naogopa mama nikimuudhi huwa mkali sana na naogopa atanibana sana nimwambie ukweli.

Usimwambie bwana tafadhali ukirudi tutafanya mpango haraka haraka hiyo mimba itolewe. Kwani upo wapi kwa sasa?

Nipo nyumba ya wageni hapa tayari nishakata tiketi kesho nakuja huko.

Na hii namba ni ya nani?

Nimemuazima huyu mkaka wa hapa guest ili nikupigie kukujulisha.

Sawa. Naomba usimwambie mama tafadhali hata akubane kiasi gani, hiyo mimba itatolewa tu.

Sawa Alex ila naomba usiniache.

Usijali Winnie nitakua na wewe bega kwa bega.

Tuliongea sana mwisho tuliagana na kukata simu.


Nilibaki na mawazo sana na kuanza kujiuliza hatima ya maisha yangu itakuaje kama Janeth na David wakija kujua kuwa mimi ndiye niliyempa Winnie ujauzito. Kiukweli nilikosa raha kabisa na kuanza kuuona mwisho wangu na David maana nilijua kwa kitendo kile asingeweza kunisamehe hata kidogo. Nilitamani hata dunia ingekua ni daladala ili nishuke maana sikutamani hata kidogo kuendelea na safari maana nilijua huko mbele sio kuzuri kabisa kwa upande wangu. Ilifika kipindi hadi nikajiona kuwa mimi ndo binadamu namba moja mwenye mawazo duniani kwani kila ninapokaa kichwa kilikua hakiwezi kusahau hata kidogo. Nilitamani sana Winfrida arudi ili tuyajenge vizuri na kuitoa mimba haraka ili kupoteza ushahidi maana nilijua wazi kua ikifahamika kuwa mimi ndo muhusika basi jela ilikua inaningoja. Siku yote hiyo nilishinda nikiwa na mawazo sana kiasi kwamba mpaka chakula nilihisi hakipiti.


Kesho yake jioni niliona ile namba ya Winnie aliyokuwa akiitumia kwa kujificha pindi anapokua yupo nyumbani ikiwa inanipigia. Sikupoteza muda haraka nikaipokea.

Hello.

Eeh Alex vipi.

Poa tu, vipi ushafika?

Ndio nipo nyumbani.

Mama umeshaonana nae?

Bado hajarudi kwenye shughuli zake hapa naogopa sana mwenzio.

Usiogope, ukiwa hivyo ndo utamfanya mama yako akubane vizuri na kunitaja.

Lakini mama mkali naogopa atanipiga.

Hatakupiga sana bwana mimi Janeth namjua vizuri.

Mimi natoroka bwana naogopa.

Hapana Winnie usifanye hiko kitu yani ndo utakua unaharibu kila kitu.

Sisi mimi nifanyaje jamani naogopa sana.

Punguza pressure na umsubiri mama arudi naamini kwa jinsi anavyokupenda hatokufanya kitu kibaya. Kama atakubana sana umwambie mtu aliyekupa mimba wewe mdanganye kuwa huyo mtu yupo Arusha na mlikuwa mnakutana kila unapoenda shule.

Mmhhh! Sasa kama akitaka kumuona je?

Naamini itakua vigumu maana Arusha sio rahisi kama hapa Dar. Na wewe kuwa mjanja kuupanga uongo ikiwezekana waambie kuwa huyo jamaa amekataa ujauzito na ametoweka pasipojulikana.

Asante Alex hapo kidogo umenipa mwanga. Ngoja niendelee kumsubiri mama lakini naogopa sana.

Pole sana ila usijali litapita tu hili.

Nashukuru sana Alex kwa kunifariji kiasi hiki maana kama ungenikataa na kuwa mkali sijui ni nani mwengine angekua bega kwa bega na mimi.


Nilimpa maneno matamu sana kumfariji huku nikizidi kumjaza ujasiri wa kuongea na mama yake pindi atakaporudi. Baada ya kuona Winnie amerizika, tuliagana na kukata simu kisha nikashusha pumzi kwa nguvu huku na mimi nikiwa na wasiwasi sana kuwa huenda Winnie atabanwa sana na kunitaja. Muda wote huo nilikaa kwa wasiwasi sana na hata nikisikia meseji ikiingia kwenye simu yangu nilikua nikishtuka sana. Hakika usiku huo ulikua mrefu sana kwangu na muda wote nilikua nasubiri kama Winnie atanipigia tena ili kunijulisha kilichotokea. Siku hiyo nilisahau hata kumtakia Vanessa usiku mwema kama ilivyokua kawaida yangu kipindi chote wakati yupo kwa shangazi yake.


*************** ***************


Siku iliyofuata wakati nipo kwenye shughuli zangu niliona Winnie akinipigia simu na nilipokea haraka haraka maana muda wote nilikua nategemea simu yake.

Winnie vipi?

Alex mambo sio mazuri hata kidogo.

Kwanini? umemuambia ukweli?

Hapana sijamwambia ila mama hanielewi hata kidogo anataka hata sasa hivi nimpeleke kwa mtu aliyenipa ujauzito maana amegundua kuwa ninamdanganya.

Aaah! Kwani wewe umemwambiaje?

Vile vile kama ulivyonifundisha lakini mama amekataa kuniamini na amenipiga sana jana.

Masikini pole sana.

(Winnie hakujibu kitu kuonyesha kuwa pole yangu isingesaidia kitu chochote kwa muda huo)

Kwahiyo leo alivyoondoka amesemaje?

Hapa ninapokwambia nipo chini ya ulinzi yani amemwambia mlinzi ahakikishe sitoki hata iweje maana anaogopa naweza nikatoroka. Jana usiku pia nililala nae kwa kuhofia hivyo hivyo na ndo maana nilishindwa kukupigia simu.

Daah! Mbona haya mambo yanazidi kukaa pabaya sasa! Sikiliza, ngoja mimi nitafute daktari mara moja kwa ajili ya kuitoa hiyo mimba.

Ila mwenzio naogopa sana, nasikia watu wengine wakitoa mimba wanakufa.

Usiogope Winnie nitahakikisha nampata dokta mzuri ili utolewe kwa uangalifu.

Sawa Alex.

Poa, baadae usiache kunitafuta basi kunijulisha kinachoendelea maana si unajua hiyo simu yako siwezi kukupigia.

Sawa usijali nitakutafuta.


Nilikata simu na kubaki najiuliza ule mtihani utapita vipi kwani hali ilishazidi kuwa mbaya. Mawazo yalinitawala sana kiasi kwamba nilijisahau kabisa kama nipo kazini hadi baadhi ya watu wakanishtukia kuwa sipo sawa. Niliingia ofisini na kukaa peke yangu na kuanza kujiuliza mustakabali wa maisha yangu utakua vipi maana ugomvi na Vanessa bado haukuisha, hatima ya mimi na Agness bado sikuijua na mauaji niliyoyafanya kwa Shaffih bado sikujua uchunguzi unaendeleaje au lile suala limeshapita. Hili la Winnie ndo lilikua linanisumbua sana kwa muda huo hadi kunikosesha raha.

Wakati nipo kwenye dimbwi zito la mawazo simu yangu ilianza kuita na nilipoitazama nilikuta ni Janeth ndo ananipigia. Moyo ulinipasuka mithili ya radi na nilianza kuogopa sana. Nilishindwa kabisa kupokea kwani niliiangalia tu ikiita hadi ikikata. Haikuchukua muda ikaanza kuita tena na nikaona huenda Janeth atanihisi vibaya hivyo ilibidi nipokee tu na kumsikiliza.

Alex vipi?

Safi tu mzima?

Ndio ila huku matatizo tu.

Matatizo gani tena hayo?

Winnie ana mimba na hivi ninavyokwambia amefukuzwa shule yupo nyumbani.

(Nilijifanya kuhamaki sana kama ndo kwanza nasikia zile taarifa wakati mimi ndo muhusika)

Nani huyo aliyempa mimba?

Nimembana sana lakini bado haninyooshei maelezo. Anadai eti kuna kijana huko huko Arusha alipokua ndo aliyempa na amemkataa na kutoweka pasipojulikana.

Mmhh! Hili tatizo.

Weacha tu. Sasa nilikua naomba jioni upitie nyumbani kwangu ili tujue tunafanyaje maana naogopa hata kumwambia baba yake huko Nairobi alipo.

(Nilishtuka sana alivyoniambia niende kwake ila sikua na jinsi zaidi ya kumkubalia ili asihisi kitu chochote kibaya)

Sawa nimekuelewa nitapitia.


Tulimaliza kuongea na kukata simu na nikajikuta nazidi kuchanganyikiwa. Kusema ukweli sikuwahi kuwa na siku mbaya kazini kama hiyo siku kwani kila kitu nilikiona kichungu kila nilipofikiria kuhusu suala la Winnie na Janeth kuniomba niende kwake.


Ilipofika jioni kwanza nilianza kurudi nyumbani ili kuoga na kubadilisha nguo ambazo zilikua na jasho sana. Sikuamini nilipofika na kumkuta Vanessa akiwa yupo jikoni anapika chakula na msichana wa kazi akiwa amempakata mtoto wangu Kelvin. Vee aliponiona aliachia tabasamu na kuanza kunifuata.......


Pole na kazi mume wangu.

Aliongea huku akinipokea briefcase na kuachia tabasamu pana usoni mwake.

Vee, umekuja saa ngapi?

Nilimuuliza huku nikionyesha kushtushwa na ule ujio wake maana sikutegemea kwa jinsi nilivyomuudhi angerudi bila ya kufanya jitihada zozote za kwenda kumbembeleza na kumuomba msamaha.

Nipo hapa tangu saa 7.

Nilimuangalia mtoto wangu Kelvin na kwenda kumchukua kutoka kwa msichana wa kazi na kumbeba. Kiasi fulani nilifarijika sana maana yale maisha ya kuwa mbali na mtoto wangu nilikua siyapendi hata kidogo.

Amina utamalizia basi hapo jikoni.

Vee alimwambia dada wa kazi na tukaelekea chumbani.

Nimekumiss sana Alex.

Hunishindi mimi Vanessa, upo sawa kweli?

Kwanini unauliza hivyo?

Kwa jinsi ulivyoondoka hapa then all of a sudden (Halafu ghafla kiasi hiki) umerudi bila hata ya kupata muda mzuri wa kukuomba msamaha.

No, i'm fine. Just let the past, just be the past (Hapana nipo sawa. Yaache yaliyopita, yabaki kuwa yamepita) Mimi sina kinyongo na wewe hata kidogo.

Really? (Kweli)

Ndio. Ila yule mshenzi sitaki tena kumuona kwenye maisha yangu. Najua kivyovyote sio wewe, ni yeye ndo aliyeanza maana ndo tabia yake kuchukua waume za watu.

Ni kweli mke wangu, ila hata mimi nilikua mjinga sana kuingia kwenye vishawishi vyake hadi kutoka nae out kwenda kunywa na kufanya huo ujinga tulioufanya. Nisamehe sana mke wangu.

Usijali mume wangu yameisha. Promise me that it won't happen again. (Niahidi kwamba haitotokea tena)

I promise you baby, it won't happen again and again. (Nakuahidi mpenzi, haitotokea tena na tena)

Nafurahi kusikia hivyo. Unajua kwanini nimerudi?

Hapana, kwanini?

Nimegundua kuwa unanipenda sana. Pamoja na kugombana lakini hukuacha kunijali, kunijulia hali na kunitakia usiku mwema kila siku. Ila jana nilivyoona kimya na hujanitakia usiku mwema nikahisi kama nakukera hivi na umechoka kuona sirudishi moyo nyuma na kukusamehe. Sio siri nilikua nafurahi sana na kufarijika pindi ukinipigia na ndo maana nimejikuta nimekusamehe kirahisi sana.

Nilitabasamu kuonyesha kufurahishwa na maneno yake matamu lakini laiti angejua kama kichwani nina stress za Winnie hata asingemaliza maneno yote hayo na hata hiyo jana yake nilishindwa kumpigia kwa sababu ya kujawa na stress na sio kama alivyodhani yeye.

Vipi shangazi hajasema chochote kuhusu hili jambo?

Kwani unafikiri hata nilimuambia? Namjua shangazi yangu yani ni lazima angetaka tuje tu huku aje kukupa maneno yako. Sijamwambia mtu yoyote, nilimdanganya tu kuwa umesafiri hivyo nimeamua kurudi kupumzika hadi utakaporudi.

That's sweet of you Vee. You are super woman. (Huo ndo uzuri wako Vee. Wewe ni mwanamke bora sana.)

Wewe nisifie tu, rudia tena halafu uone.

Utafanya nini?

Wewe rudia tu ndo utajua.

Basi mke wangu yaishe sirudii tena.

Ila yule malaya wa kike bado sijamalizana nae, haiwezekani nimuangalie tu ataona namuogopa. Lazima nimfundishe adabu aache kuparamia mabwana za watu.

Mhh! Baby kama umeamua kusamehe wewe samehe kila kitu. Mchukulie ni malaya tu kama unavyosema na ukae nae mbali kabisa maana hatutakii mema kwenye mahusiano yetu.

Halafu unavyonishauri utasema wewe hauhusiki vile kumbe na wewe upo humo humo.

Baby! basi tuache kuongea haya.

Sio tuache, mimi lazima nimfundishe adabu yule labda akajifiche sijui wapi nisipopajua.

Mmhh haya, kuwa makini tu.


Tuliongea mambo mengine mengi sana na kumshukuru kwa kunisamehe na kurudi nyumbani ili tumlee mtoto wetu pamoja.

Baby ngoja nijiandae nataka nitoke mara moja.

Unaenda wapi tena jamani wakati mwenzio nimekumiss?

Naenda nyumbani kwa David, wameniita kuna jambo la muhimu sana tunaenda kuongea.

Bwana! mwenzio nitabaki nimeboreka hapa.

Pole mke wangu ila usijali sichelewi kurudi ni mara moja tu.

Aliniangalia kwa macho yake ya kudeka na sura iliyojaa mapozi kisha akanilalia mapajani.

Sawa, uwahi basi leo silali hadi unikate kiu yangu maana nimekumiss sana.

Sawa baby usijali tena ujiandae maana hata mimi nimekumiss sana na nina hamu sana na wewe.

Nilimjibu huku nikimchezea nywele zake kichwani.


Baada ya kumuona Vee ameridhika, niliingia chooni kuoga haraka haraka na kujiandaa kisha nikamuaga Vanessa na kumpiga mabusu kadhaa ya mdomoni ambapo alifurahi sana. Nilianza safari huku kichwani nikiwa na mawazo sana ni jinsi gani ile kesi itapita maana Janeth alikua anataka kumjua kwa udi na uvumba huyo aliyempa mimba mtoto wake. Baada ya mwendo wa takribani dakika 30 kutoka Mbezi ya Kimara hadi Mbezi beach niliweza kufika salama. Nilipiga honi na kufunguliwa geti na mlinzi kisha nikaingiza gari ndani. Nilisalimiana na mlinzi kisha nikaanza kuingia ndani sebuleni. Niligonga hodi na kusikia sauti ya Janeth akinikaribisha. Nilifungua mlango na kuingia ndani ambapo nilimkuta Janeth akiwa yupo peke yake anaangalia TV.

Alex vipi za tangu mchana?

Nzuri tu, vipi za hapa?

Za hapa kama unavyojua hali si shwari. Mdogo wako Winnie kashaharibu na shule amefukuzwa.

Nilionyesha kusikitika sana kumbe mimi mwenyewe ndo mubusika wa ule uharibifu.

Kwahiyo shule wamesemaje?

Hawamtaki tena yani amefukuzwa. Sheria ya shule mtoto akipata mimba basi anafukuzwa na haruhusiwa tena kurudi hata iweje yani.

Dah! sio mchezo. Winnie mwenyewe yuko wapi?

Yupo huko ndani chumbani kwake.

Aliongea Janeth na kuanza kupaza sauti yake kumuita Winnie. Baada ya kuita takribani mara nne nilisikia Winnie akiitikia na baada ya kama dakika tatu alitokea huku akionyesha kuwa mnyonge sana.

Shikamoo kaka Alex.

Marahaba, mambo vipi?

Poa.

Winnie aliitikia kwa unyonge sana. Siku zote pindi tunapokua mbele ya Janeth au David, mimi ma Winnie huwa tunaheshimiana sana na huwa ananiamkia.

Dada yako yuko wapi?

Janeth aliuliza swali lililonishtua sana kwani nilijua moja kwa moja atakua ni Happy tu naye amekuja.

Atakua yupo chumbani kwake.

Hebu nenda ukamuite.

Winnie aliondoka kwa unyonge sana na Janeth alimtazama kwa hasira.

Yani mtoto kanikera huyu hata sijui nimfanye nini.

Punguza hasira, waswahili wanasema mtoto akijisaidia kwenye kiganja haukikati ila unakiosha na maisha yanaendelea.

Mmh! Ila kwa hili hapana amejua kunitibua.

Nilikua naongea na Janeth lakini akili yangu ikiwa haipo sawa hata kidogo kwani nilihisi ule uwepo wa Happy unaweza ukafanya mambo yaende tofauti na nilivyoyapanga. Kweli baada ya kama dakika tano nilimuona Winnie akirudi na nyuma yake yupo Happy. Nikamuona Happy akinikata jicho kali sana lenye kuashiria hali si shwari na aliniogopesha sana.

Mambo.

Alinisalimia bila kuonyesha uchangamfu na mimi nikamuitikia vizuri tu.


Tulikaa kimya kwa muda wa kama dakika moja kila mtu akiwa anawaza kwa upande wake na mara Janeth akavunja ukimya.

Alex nimekuita hapa naamini wewe ni kama kaka kwenye familia hii na unaweza kuwa na lolote la kuongea juu ya haya yaliyotokea kwa Winnie. Nafikiri nimeshakueleza na unafahamu kila kitu. Happy na wewe nilikupigia na ukasema kwenye simu hauwezi kusema chochote mpaka tukikutana na ukasema ni vizuri Alex awepo. Haya umekuja na Alex huyu hapa. Una lipi la kusema juu ya huu ujinga alioufanya mdogo wako?


Kitendo cha Janeth kuongea hivyo na kumpa Happy nafasi ya kuongea kilinifanya nihisi kama tumbo la kuhara likianza kunikata na lile sofa nililokaa nianze kuliona linawaka moto. Mapigo ya moyo yaliongezeka maradufu na kujikuta nikianza kuhisi joto ingawa mahali hapo palikua na A.C inayofanya kazi vizuri sana......



Happy alivuta pumzi ndani na kuzitoa nje kwa nguvu na kututazama wote tuliokuwepo pale.

Winnie unasema mwanaume aliyekupa hiyo mimba yupo wapi?

Happy aliuliza huku akionyesha kuwa yupo serious sana.

Yupo Arusha.

Huyo mwanaume ilikuwaje ukakutana nae na Arusha muda wote unakua upo shule?

Nilikutana nae likizo ya mwaka jana mwezi wa sita wakati nilipoenda sokoni na marafiki zangu kununua vifaa vya shule na vitu vyengine.

Happy aliguna kidogo kisha akaendelea.

Kwahiyo umeanza lini kukutana nae kimwili?

Winnie alikaa kimya kidogo kuonyesha kuwa hilo swali lilikua gumu kwake kujibu.

Si nakuuliza wewe? Mara ya kwanza mlilala lini?

Mwaka jana mwishoni.

Winnie alijibu kwa unyonge sana huku na mimi nikiwa makini na muoga sana kusikiliza Winnie asiharibu mambo.

Huyo mwanaume anafanya nini kwa sasa na ana umri gani?

Sijui anachofanya ila sio mkubwa.

Hujui? Ina maana tangu mwaka jana unajuana nae haujajua kazi yake au shughuli yoyote anayofanya.

Ndio sijawahi kumuuliza.

Mama huyu mwanao nahisi anatudanganya hiki anachokisema sio cha kweli.

Happy alikua anaongea kama dada haswa na alionyesha kuwa serious sana kiasi kwamba hata sikuamini kama ndo yeye.

Wewe Winnie hebu sema ukweli kabla sijakubadilikia kama jana. Tuambie huyo mtu anapoishi tena twende wote utupeleke.

Janeth nae aliongea kwa ukali sana.


Pamoja na vitisho vyote hivyo Winnie hakuongea kitu chochote cha ziada na alibaki na msimamo wake ule ule. Muda wote huo nilikua kimya na nilishindwa kuchangia kitu chochote.

Mama kuna kitu nakihisi ila sijui kama kina ukweli.

Aliongea Happy huku akimtazama mama yake usoni.

Kitu gani hiko?

Nahisi huyo mtu tunayemtafuta wala anaweza asiwe mbali kama Winnie anavyotujibu.

Nilihisi moyo wangu ukipasuka vipande vipande na mwili kunyong'onyea sana. Nikajua sasa Happy anataka kumwaga mchele kwenye kuku wengi na kuharibu kila kitu.

Kwanini unasema hivyo.

Haya majibu ya Winnie hayaniingii akilini hata kidogo nikijumlisha na vitu ambavyo mimi navijua.

Vitu gani hivyo hebu niambie.

Sasa nikabaki kama vile ngamia aliyesomewa na kuelekea kibla yani nilikua nasubiri kuchinjwa tu.

Kwanza kabisa naomba unisamehe sana mama yangu kwa haya nitakayoanza kukwambia maana najua nimekosea sana.

Hebu ongea bwana Happy mbona unazunguka sana?

Janeth aliongea huku akionyesha kuwa na uchu sana na kitu ambacho Happy anataka kusema. Kweli Happy nae hakujivunga kwani akaanza rasmi kuumwaga mchele wote.

Kipindi kirefu sana wakati Alex anaishi hapa nyumbani tulikua wapenzi.

Eeeeee!!! Niniiiii!!!?

Nisamehe sana mama yangu, najua nimekosa sana.

Muda huo kidume kijasho chembamba kilikua kinanichuruzika utadhani nimewekwa katikati ya jua la utosi.

Wewe Happy, unasema nini!!??

Mimi na Alex tulikua wapenzi.

Mungu wangu!! Alexxx!!!!

Janeth aliniita kwa uchungu sana huku nikimuona sura ikianza kubadilika na kutaka kulia. Nilishindwa hata kuitikia nikabaki naangalia chini tu. Happy akaendelea kuhadithia huku na yeye kama akianza kulia kwa mbali.

Nilitokea kumpenda sana Alex na ilifika kipindi nikahisi huenda tukaja kuoana maana tulikaa muda mrefu kidogo. Na hata alivyohama pia tuliendelea japo kidogo kasi ilipungua. Nakumbuka siku niliyokuja kumchukia vibaya sana na kuapa kuwa sitokuja kumsamehe ni siku niliyowakuta live yeye na Winnie wakiwa wamezama kwenye mapenzi wanabadilishana mate.

Unasemaaaa!!!?

Janeth alizidi kupigwa na butwaa na kuanza kulia.

Ndio na baadae nilikuja kumbana Winnie na akakiri kweli kuwa yeye na Alex ni wapenzi na tayari wameshakutana kimwili.

Alexxx!!! Hivi wewe ni mnyama kiasi hiko!!!?

Janeth aliongea kwa ghadhabu sana huku akiwa analia na ghafla nikamuona anainuka na kuja kunivamia na kuanza kunirushia makonde ya nguvu. Nilijitahidi kumzuia na kumkwepa lakini mengine yalikua yananipata vizuri.

Shemeji!! shemeji naomba unisikilize tafadhali!!

Niliongea kutaka kujitetea lakini kiukweli sikuwa na neno lolote la maana ambalo ningeweza kuongea na kueleweka.

Tulia malaya mkubwa wewe!! Ina maana.....Aaahh!!! Kwelii!!??

Janeth alitaka kuongea juu ya kitendo nilichofanya cha kumchanganya yeye na watoto wake lakini alishindwa kabisa.


Huyu mshenzi ndo amempa mwanangu mimba.

Janeth aliongea kwa jazba sana huku akizidi kunirushia makonde hadi nikaona nguvu zikimuishia na kuanguka chini na kuanza kuangusha kilio cha kufa mtu.

Wewe Winnie sema ukweli hiyo mimba ni ya Alex au sio yake?

Happy aliuliza akionyesha kuwa serious sana.

Winnie alikua kimya huku taratibu nikimuona akianza kulia.

Semaa!! malaya mkubwa wewe. Mtoto mdogo hata form four hujamaliza lakini umeshaanza tabia za umalaya. Niambie hiyo mimba ni ya nani?

Winnie hakusema kitu zaidi ya kuanza kulia tu.

Mara nikaona Happy akimvamia Winnie na kuanza kumpiga makofi yasiyokua na idadi yaliyomfanya Winnie alie kama mtoto mdogo.

Nisamehe dada!!

Semaa, mshenzi wewe!!

Niache dada nakwambia.

Kweli Happy akamuacha huku akitweta kwa jasho jingi sana na kuhema kwa kasi.

Niambie sasa, ni nani huyo?

Winnie alishindwa kabisa kuongea na kuendelea kulia tu kitendo kilichofanya Happy aendelee kumpa dozi bila kujali sehemu anazompiga.

Basi dada nisamehe, nakwambia.

Semaa!! malaya mkubwa wewe!!

Winnie aliendelea kulia na kunitazama usoni ambapo nilitamani hata nigeuke upepo na kupotea haraka mahali pale.

Mimba ni ya Alex!

Sio siri katika maisha yangu hakuna sio niliyojihisi kufedheheka, kukosa thamani, na sistahili kuitwa mtu mbele za watu kama hiyo siku kwani nilishindwa hata kunyanyuka kwenye sofa na mwili ulikosa nguvu kabisa.

Mama si unaona!! Si nilisema kuwa huyo mtu tunayemtafuta anaweza hata asiwe mbali?

Happy aliongea kwa kujiamini sana na sikuamini hata kidogo kama ni yeye ndo alikua ananikandamiza kiasi kile.

Alex nakufunga, lazima nikufunge Alex!!

Janeth aliongea kwa jazba sana huku akiwa analia kwa uchungu kupita maelezo.

Naomba unisamehe shemeji!

Wee! tena nyamaza, malaya mkubwa wewe. Lazima ukaozee jela siwezi nikakuacha.

Muda huo kilichotawala hapo ni vilio tu, Happy peke yake ndo alikua halii ila alionekana kuwa na hasira mithili ya mbogo. Nilijitahidi kuanza kuinuka na kuondoka huku nikiwa mnyonge sana.

Tena hiyo funguo ya gari iweke hapo. Tumekuthamini na kukupa kila kitu ila leo hii ndo malipo yake haya.!!!

Janeth alikua anaongea kwa uchungu sana na bila kubisha kinyonge sana nikaiweka funguo ya gari mezani. Nikaanza kutoka nje na kuondoka taratibu kwa miguu kuelekea vituo vya daladala. Kichwani nilikua na mawazo yasiyokua na idadi kiasi kwamba nilikua hata sioni mbele ninapokwenda.


Nilirudi nyumbani na nilivyofika Vee alinishangaa sana kurudi bila gari.

Vipi mbona umerudi hivyo gari umeliacha wapi?

Nilimtazama kivivu sana jinsi mawazo yalivyonielemea.

Limeharibika hivyo nimeliacha huko huko.

Nilimjibu kwa ufupi tu ili asiniulize tena maana kwa jinsi kichwa kilivyovurugika, sikutaka hata kidogo maswali yaendelee.

Ooh! sawa, pole.

Asante. Naomba nikapumzike Vee akili yangu haipo sawa hata kidogo.

Kwanini? Na pia si unakumbuka nilivyokwambia wakati unaondoka? Sasa unaenda kulala vipi?

Sipo sawa hata kidogo hivyo naomba unielewe tu na uniache nikalale.

Sitaki bwana mimi nakutaka wewe hapo.

Laiti kama Vanessa angejua hali niliyokua nayo hata asingeendelea kuniongelesha na angeniacha tu nikalale. Nikaamua nimuache na kuingia chumbani ambapo nilijitupa kitandani hata nguo sijabadilisha.

Baby una nini lakini mbona umekua hivyo?

Vee, naomba tuepushe huu ugomvi na kutoelewana, naomba kwa wakati huu uniache na usiniongeleshe.

Vee alinitazama kwa jicho la ukali sana na akatoka chumbani kwa ghadhabu sana na kuufunga mlango kwa nguvu. Sikujali, nilijilaza na kuanza kutafakari kila kitu kilichotokea nyumbani kwa David.

Mawazo yalinitawala sana kiasi kwamba hata sijui nilikuja kupitiwa na usingizi saa ngapi.


Kesho yake niliamka na kujikuta napata wazo la kumuibia David pesa zake nyingi za kwenye biashara yake kisha nikimbie mbali maana nilishaona kuwa mwisho wangu na David pamoja na familia yake ulikua umefika. Pia niliiona hatari ya kwenda kuozea jela maana Janeth alishaapa kuwa ni lazima atanifunga. Kweli nikaanza kupitia biashara zote za David na kukusanya pesa ambapo mpaka namaliza nilijikuta nina takribani milioni 33 na nusu ambazo kwa kawaida huwa naenda kuziweka benki. Nikazitia kwenye begi la mgongoni nililolibeba siku hiyo na kuchukua kila kitu kinachonihusu ofisini hapo maana nilijua fika kuwa sitorudi tena. Nilikodi tax na kurudi nyumbani ambako Vanessa sikumkuta japo alikua yupo likizo. Nikapanga kuwa niende mkoani Mbeya kujichimbia huko huku Vee nikiwaacha na mtoto nyumbani kwangu maana sikutaka kuwatia matatizoni haswa mtoto wangu. Ila kwanza nilipanga kwenda Tanga kijijini kwetu ili nikamuone Aggy na kumwambia kuhusu mpango wangu wa kurudiana nae na ikiwezekana niondoke nae tukaishi Mbeya kama nilivyopanga.

Kweli siku hiyo hiyo sikulaza damu, nilibeba baadhi ya nguo zangu na kuondoka bila kumuaga Vee na kwenda stendi ya mabasi Ubungo kwa ajili ya safari ya kuelekea Tanga.


Kwanza nilipitia benki ambapo nusu ya zile hela niliziweka kwenye akaunti yangu ambayo niliifungua takribani miezi nane iliyopita ukiachana na ile akaunti aliyonifungulia David mara ya kwanza wakati ndo naanza kazi kwake. Mchana yapata saa 8 basi lilianza safari huku nikiwa na shauku kubwa ya kufika na kuonana na Agness.............





Njiani nilikua na mawazo sana juu ya mustakabali mzima wa maisha yangu na nikajiona mjinga sana kwa makosa yote niliyoyafanya. Baada ya safari ya takribani masaa 6, tuliingia Tanga mjini mishale ya saa 2 usiku. Kwa kuwa magari ya kwenda kijijini kwetu mwisho ni saa 10 jioni, ilinilazimu nikakodi chumba hotel ili kesho yake asubuhi na mapema nielekee kijijini kwetu. Kweli nilipata chumba kwenye hotel moja nzuri iliyokua na ulinzi mzuri sana maeneo ya Garden kama unapafahamu Tanga mjini.

Kesho yake asubuhi na mapema baada tu ya kupata kifungua kinywa nikaanza safari ya kuelekea stendi kwa ajili ya gari za kuelekea kijijini kwetu. Mishale ya saa 5 asubuhi nilifika salama nyumbani ambapo nilimkuta mama akiwa yupo nje barazani.

Alex, ndo wewe baba?

Ndo mimi mama, shikamoo.

Marahaba, vipi wote wazima huko mwanao pamoja na mzazi mwenzio?

Ndio wote hawajambo kabisa.

Mbona umekuja ghafla kiasi hiki tena sio wikiendi kama kawaida yako?

Dharura tu mama. Pia nimekuja kuonana na Agness nimepata taarifa zake kuwa yupo hapa kijijini.

Wee! yupo tangu lini?

Sijajua ila ni James ndo alinipa taarifa hivi juzi juzi alivyokuja huku.

Ndio James nimeonana nae alikuja mpaka hapa ila hakuniambia kuhusu habari za Agness.

Basi ndo hivi nasikia amerudi yule mume wake aliyemuoa alifariki.

Wee! lini hiyo?

Hata sijui mimi mwenyewe nimepewa taarifa juzi juzi tu hapa.

Sikutaka kuongea mambo mengi ili nisije kujikanyaga na mama akaanza kunihisi pengine nahusika kwa namna yoyote na tukio hilo.

Masikini, kwahiyo Agness ameamua kurudi kwa mama yake tu.

Ndio, hivi nimekuja kwa ajili yake nataka nikaongee nae.

Sawa mwanangu, naamini atakuelewa tu na kukusamehe kwa jinsi alivyokua anakupenda.

Nashukuru sana mama kwa kunitia moyo.

Tuliongea mambo mengi sana hususani kuhusu mtoto wangu Kelvin pamoja na mustakabali juu yangu na Vanessa. Nilimueleza kila kitu kuwa ndoto yangu ni kuishi na Agness ila kama itashindikana basi nitabaki na Vanessa tu.


Niliingia ndani na kuweka mabegi yangu huku lile lenye hela nikilificha mbali sana ambapo sio rahisi kwa mtu kuingia na kuliona mara moja. Nilijiuliza sana nikienda kwa Aggy niingie kwa gia gani ili anipokee na kuweza kunielewa. Zilishapita takribani wiki tatu sasa na ulikaribia mwezi tangu nifanye lile tukio la kumuua mume wake Shaffih na nikaamini kuwa hakuna kesi inayoendelea na wala isingekua rahisi kutambulika kwa jinsi mazingira yalivyokua.

Ilivyofika mida ya saa tisa alasiri nikaanza kujongea taratibu kuelekea nyumbani kwa kina Agness huku mapigo ya moyo yakizidi kuongezeka kwa hofu niliyokua nayo. Nilifika na kwa bahati nzuri nilimkuta Halima akiwa na msichana mwengine ambaye nilikua nikimuona tu pale kijijini tangu zamani lakini hata sikumjua jina lake.

Hee! Alex umekuja!! Karibu.

Halima alinikaribisha kwa uchangamfu sana kama kawaida yake.

Asante sana Halima, vipi habari zenu.

Nzuri, sijui wewe.

Waliitikia na kuniuliza wote kwa pamoja.

Safi tu. Halima unaendeleaje?

Niko poa kama unavyoniona ila matatizo tu ndo yametuandama.

Matatizo gani tena hayo?

Wiki iliyopita tu nimetoka kufiwa na bibi yangu mzaa mama na kuhusu Agness nafikiri tayari taarifa umeshazipata.

Aisee, pole sana kwa msiba wa bibi.

Asante nimeshapoa.

Kuhusu Agness ni kweli taarifa ninazo aliniambia yule rafiki yangu James.

Ooh! Halafu nilionana nae kama sikosei wiki iliyopita.

Ndio alikuja huku mara moja ila tayari ameshaondoka.

Sawa. Eenhe! lete story.

Vipi Agness na mama yake wapo?

Mama hayupo ila Agness yupo ndani, si unajua bado hajamaliza eda?

Aanha sawa. Ila nimekuja kwa ajili yake na nina shida sana ya kuongea nae.

Mmhh! Naogopa usije ukamfanya shoga yangu aanze kuangusha kilio saa hizi maana hayupo sawa hata kidogo na ukimuona amekonda sana hutoweza kuamini.

Tafadhali naomba unisaidie Halima ni muhimu sana kwani nina mambo machache sana ya kuongea nae.

Hapana mimi naogopa bwana, najua lazima utamtibua shoga yangu.

Tafadhali Halima nisaidie sana nipo chini ya miguu yako.

Nilikuwa naongea kwa unyonge sana huku yule msichana mwengine akiwa yupo makini kuniangalia.

Halima alikaa kimya kwa muda akiwa anatafakari achukue maamuzi gani.


Wakati ukimya ukiwa umetawala, ghafla tulisikia sauti ya Agness kutokea ndani akiwa anamuita Halima. Moyo ulishtuka sana kusikia sauti yake na nilibaki kimya nikiwa namtazama Halima. Halima aliinuka na kuelekea ndani ambako baada ya kama dakika tano nilimuona akitoka na kusimama mlangoni huku akinionyesha ishara kuwa nimfuate kule ndani. Kweli sikujivunga, niliinuka haraka haraka na kuanza kuelekea ndani na kumuacha yule msichana mwengine pale pale kwenye mkeka.

Nasra nisubiri hapo hapo shoga yangu usiondoke.

Halima alimwambia yule msichana ambaye alimjibu kuwa amemuelewa. Tuliingia mpaka ndani na kumkuta Agness akiwa amejifunika kanga mpaka kichwani na alionekana sehemu ya sura yake tu.

Agness, pole sana kwa matatizo yote haya unayopitia.

Niliongea huku nikikaa chini kabisa sakafuni.

Asante.

Alijibu kwa sauti iliyokauka kama vile mtu aliyetoka kulia sana.

Nilipata taarifa kutoka kwa James hivi juzi juzi alikuja huku kijijini.

Sawa, ndo hivyo.

Pole sana, hakika imenigusa sana na ndo maana leo unaniona nipo hapa.

Aggy alikaa kimya tu huku akiwa anaangalia chini.

Vipi wewe mwenyewe unavyoendelea?

Sijambo naendelea vizuri.

Sio kweli Aggy, unaendelea vizuri wakati unazidi kudhoofu kiasi hiko?

Aggy aliinua shingo yake ni kuniangalia usoni kama vile mtu anayetaka kusema kitu lakini alikaa kimya tu.

Nakuonea huruma sana Aggy kwa umri uliokua nao na mambo yote hayo mazito unayopitia. Sio siri moyo wangu unaniuma sana kukuona ukiwa kwenye hali hiyo.

Usijali nitakua sawa tu.

Lini sasa na kila siku nasikia upo hivyo hivyo na unazidi kudhoofika?

Alex naomba tuache kuongea hayo na ufate kilichokuleta.

Aggy aliongea kwa sauti ya chini lakini yenye kuonyesha msisitizo.

Mimi nimekuja lengo langu ni moja tu, naomba unisamehe kwa yote Agness na turudi kama zamani. Hakika wewe ndo furaha yangu bila wewe siwezi kabisa na namiini hata wewe mwenyewe utakua umeliona hilo. Japokua ulikua umeolewa, sikuacha kukupigania na kugombama sana na marehemu mume wako na yote hiyo ni juu ya mapenzi mazito niliyonayo kwako. Nakupenda sana Agness na kamwe sitoacha kukupenda mpaka naingia kaburini.

Alex tafadhali nakuomba usiongee habari za mapenzi sitaki hata kuzisikia.

Lakini nakupenda Aggy nitaachaje kuongea?

Nimesema sitaki Alex.


Ghafla nikamuona Aggy akianza kulia kama vile mtu aliyetoneshwa kidonda chake.

Alex naomba uondoke tafadhali Aggy ana msongo wa mawazo sana na hapa ndo unazidi kumchanganya.

Aliongea Halima ambaye alikua yupo pembeni yetu.

Hapana Halima siwezi kuondoka mpaka nitakapohakikisha Aggy amekubali kurudi kwangu.

Sawa ila sio kwa wakati huu hivyo naomba uondoke.

Mara nikaona kilio cha Aggy kikizidi kuongezeka maradufu hadi nikashangaa ni kitu gani kinachomliza kiasi hiko.

Agness vipi mpenzi mbona hivyo tena?

Nilimuuliza kwa hofu sana huku nikiwa nimemsogelea karibu kabisa.

Kwanini Alex, kwaninii??

Kwanini kitu gani?

Kwanini kila siku unaniumiza mimi tu Alex?

Mhh! Mbona mimi sijafanya kitu mpenzi wangu.

Najua kila kitu Alex ukweli wote umeshafahamika.

Ukweli kuhusu nini.

Niliona Aggy ananiacha njia panda kwani alikua anaongea vitu ambavyo hata sivielewi.

Umemuua mume wangu Alex.!!!

Aggy aliongea kwa uchungu sana na kilio kuzidi maradufu mara mbili ya mwanzo. Kusema ukweli nilishtuka sana Aggy atakua amepata wapi hizo habari maana nina uhakika hakuna mtu yeyote aliyeniona wakati nafanya lile tukio.

Aggy hebu acha masihara bwana, nimuue mume wako kwa sababu ipi sasa?

Hauna cha kujitetea Alex ushahidi wote upo wazi na video nimeiona. Ni wewe kabisa.

Video? una maana gani unaposema hivyo?

Eneo ulilofanya mauaji kuna nyumba imefungwa camera imenasa tukio lote na hivi ninavyokwambia unatafutwa sana na polisi.

Nilihisi kama mwili sio wa kwangu jinsi ulivyoishiwa nguvu na kunyong'onyea.

Hapana Agness mimi sijafanya hivyo.

Alex hauwezi ukaniambia kitu nimeona video yote na sura yako imeonekana kabisa. Kwanini lakini umekatisha uhai wa Shaffih? Kwanini umezidi kuniumiza? Hivi unajua kama wazazi wake walikua wanamtegemea nyumbani kwao? Kwanini lakini, kwanini!?? Kwanini umekua katili kiasi hiko Alex? Dar imekufanya nini hadi umekua hivi?

Aggy alikua anaongea huku akiwa analia sana. Sio siri nilishindwa hata kujitetea na bila kutegemea nikajikuta na mimi nikianza kuangusha kilio kizito sana.

Agness nisamehe sana mpenzi wangu, sio mimi ni shetani tu ndo alinipitia. Nakupenda sana Agness na niliona kufanya hivyo ndo njia pekee ya kukurudisha mikononi mwangu.

Hapana Alex ndo umezidi kuharibu. Umeharibu sana Alex. Shaffih alikua ni mtu mwema sana na anayemjua Mungu. Kwanini umeyachukua maisha yake?

Muda huo Halima nae pembeni alikua analia sana huku akifatilia vizuri maongezi yetu.


Nilibaki nalia sana na sikua hata na kitu cha kujitetea.

Aggy naomba unisamehe mimi, naomba unisamehe!! Nimekuumiza sana mpenzi wangu.

Muda huo Agness alikua analia sana na hawezi hata kuongea vizuri.

Alex naomba uondoke haraka kwani muda wowote kutoka sasa maaskari wanaweza kufika hapa.

Maaskari? Wamejuaje kama nipo hapa.

Niliuliza kwa mshangao sana.

Maaskari wamekuja sana hapa kutaka ushirikiano na mimi na wameniomba pindi nitakapokuona mahali popote pale basi niwape taarifa. Wakati nilipokusikia nje umekuja nilijikuta nimewatumia meseji bila kutegemea kwa hasira nilizokua nazo. Tafadhali naomba uondoke Alex na ukimbie mbali sana. Sitaki niishi nikijiona mwenye hatia kwa kusababisha kukamatwa kwako. Naomba uondoke haraka sana na nisikuone tena kwenye maisha yangu. Nakupenda sana Alex tangu siku ya kwanza nilipokuona na upendo wangu kwako kamwe hautokuja kuisha hata iweje. Nitakupenda sana kwa kipindi chote cha maisha yangu ila siwezi tena kuwa na wewe.

Maneno ya Aggy yalikua ni kama mkuki wa moto sana unaopenya katikati ya moyo wangu kwani yaliniumiza sana na kunifanya nilie mithili ya mtoto mdogo. Nililia sana kiasi kwamba nilishindwa hata kuongea.

Alex naomba uondoke maaskari wanakaribia, tafadhali naomba uinuke uondoke.

Nikaanza kutafakari suala la kuishi maisha yangu yote yaliyobaki nyuma ya nondo na nikaona ni suala ambalo haliwezekani hata kidogo.

Ina maana hii ndo HATIMA YA MAPENZI yetu mimi na wewe Agness? Ina maana mimi na wewe ndo basi tena?

Agness alikua analia sana kiasi kwamba alishindwa hata kunijibu.

Sawa mimi naondoka, ila siku zote za maisha yangu utaishi moyoni mwangu. Nakupenda sana Agness na jua kwamba napitia yote haya kwa sababu yako. Nimeua kwa sababu yako na nitaenda jela kwa sababu yako. Kwaheri Agness!!

Niliongea kwa uchungu sana na kuanza kutoka nje na kuondoka kinyonge sana.


Wakati nipo njiani nakaribia nyumbani niliiona defender ya polisi ikiwa inaelekea njia inayoenda nyumbani kwa kina Agness kwa kasi sana. Nilijibanza kwenye kibanda na kuingoja mpaka ilipopotea kabisa na nilianza kutoka mbio kuelekea nyumbani.....



Nilikimbia sana na sikuchelewa kufika. Niliingia mpaka ndani na kumshtua sana mama aliyekua anaangalia TV.

Vipi Alex mbona umerudi mbio hivyo kama unakimbizwa?

Mama nimekwisha mimi, nimekwisha.

Umekwisha? umekwisha kitu gani?

Nilishindwa hata kumjibu na haraka nikawahi chumbani kuchukua vitu vyangu. Nilimsikia mama akigonga hodi lakini sikumjibu. Sikukawia, haraka haraka nilitoka na kurudi sebuleni na mama akanifuata nyuma.

Alex una nini lakini mbona unanichanganya kiasi hiki?

Sikumjibu kitu, nilifungua begi lililokua na hela na kutoa vibunda vitano ambavyo kila kimoja kilikua na shilingi milioni moja.

Mama, kama hatutopata bahati ya kuonana tena, hizi zitakusaidia kuanza maisha bila mimi.

Alex umepatwa na kitu gani mwanangu mbona unanichanganya mimi mama yako?

Mama aliongea kwa uchungu sana huku nikimuona kabisa akiwa anataka kulia.

Nafikiri sina muda wa kutosha mama kukueleza kila kitu, nikipata bahati ya kuonana tena na wewe nitakwambia kila kitu.

Alex baba, nini kimekupata mwanangu? Umefanya nini?

Nilimuangalia mama kwa uchungu sana hadi machozi yakaanza kunitoka. Sikuweza kujizuia hata kidogo hadi nikajikuta ninamsogelea mama na kwenda kumkumbatia.

Nipo kwenye wakati mgumu sana mama naomba uniombee mwanao. Ila chochote kitakachotokea kaa ukijua kuwa mwanao ninakupenda sana. Nakupenda sana mama yangu.

Baada ya kumaliza kuongea maneno hayo nilimuachia na kubeba mabegi yangu na kuanza kuondoka maana nilihisi maaskari huenda wangekuja mpaka nyumbani kwetu tu maana Agness alishawapa taarifa kuwa nipo pale kijijini.

Alex mwanangu, Alex!

Mama aliniita kwa uchungu sana kiasi kwamba sikutaka hata kugeuka kuitazama sura yake maana najua ningezidi kuumia. Nilitoka mpaka nje na kuanza kutembea kwa haraka sana ambapo sikupita njia ya kawaida iliyozoeleka na watu wengi kwa kuhofia kuwa huenda wale maaskari wakaniona. Nilipita njia za msituni sana kwani nilikua mwenyeji na mzoefu wa njia hizo tangu wakati nipo mdogo.


Nilitembea sana mpaka nikafika kijiji kingine. Kwa bahati mbaya kijiji hiko hakikuwa na wakazi wengi hivyo hata suala la usafiri lilikua la shida sana kwani magari yalikua hayafiki. Laiti kama watu niliokua napishana nao wangejua kuwa lile begi nililobeba lilikua na zaidi ya milioni kumi, basi ni lazima wangenivamia tu. Nilipita kijiji hiko na kuzidi kutembea kuelekea kijiji kingine cha mbele ambako kidogo nilijua pamechangamka na hata suala la usafiri halikua linasumbua sana. Nilitembea sana pori kwa pori huku nikiwa nimejawa na uoga sana, kwanza kwa kuhofia kukamatwa na polisi na pili kuhofia kuvamiwa na wezi au majambazi. Baada ya mwendo wa zaidi ya nusu saa, nilifanikiwa kufika kwenye kijiji cha Zingibari ambapo nilikuta kumechangamka sana zaidi ya miaka ya nyuma mara ya mwisho nilivyoenda. Nikawa najiuliza usafiri wa kwenda mjini unapatikana wapi maana palikua pamebadilika sana. Nilimuona kijana mmoja ambaye nilihisi hatujapishana sana umri na nikaamua kwenda kumuuliza.

Mambo vipi.

Poa, vipi wewe?

Safi tu. Samahani ndugu yangu mimi ni mgeni hapa nilikua nauliza gari za kwenda mjini zinapatikana wapi?

Wewe unatokea wapi kwani?

Natokea kijiji cha Loko kuna jamaa tuliahidiana kukutana huku lakini mpaka sasa simu yake haipatikani. Nililetwa na pikipiki tu huku.

Ilinibidi kudanganya ili mambo yasizidi kuwa mengi. Kweli yule jamaa aliweza kunielewa vizuri.

Umeuona ule mnara wa simu kule mbele?

Ndio nimeuona.

Sasa ukifika pale pita njia ya kushoto kuna fundi baiskeli. Nyoosha mbele utaona kiwanja cha mpira. Ukikimaliza tu utaona mtaa wa kwanza kabisa unaingia kulia. Pita hapo mbele yake tu utaona kuna gari ndogo, ndo hizo hizo ulizia tu.

Sawa ndugu yangu nimekuelewa shukrani sana.

Sawa karibu sana.


Baada ya kueleweshwa vizuri, nilianza kuondoka kwa mwendo wa haraka kama kawaida na baada ya muda mfupi nilifika na kuzikuta gari tatu aina ya Noah zikiwa zinapakia abiria.

Vipi mjomba, njoo ya kuwahi hii hapa.

Aliongea jamaa mmoja ambaye nilihisi ni mpiga debe wa eneo lile.

Si zinaenda Tanga mjini hizi?

Ndio, unapelekwa mpaka stendi barabara ya 12.

Sawa, inaondoka saa ngapi?

Sasa hivi tu, ukiingia wewe wanabaki watu wawili chap kwa haraka.

Yule jamaa alionekana kuipamba sana kazi yake.

Niliingia kwenye gari na kukaa nyuma kabisa. Kweli baada ya kusubiri kama dakika 20, gari ilijaa na kuanza kuondoka. Muda huo nilitamani hata tuwe tumeshafika Tanga mjini na kupanda basi la kurudi Dar maana Tanga haikua sehemu salama tena kwangu. Gari ilitembea kwa kasi sana kiasi kwamba ilifika sehemu trafiki akaisimamisha. Dereva alishuka na kwenda kuongea nae kama dakika tatu hivi. Nilishtuka sana nilipoona yule trafiki anakuja na kufungua mlango wa gari na kuchungulia ndani kututazama abiria wote.

Habari za saa hizi jamani.

Kila abiria mule alimjibu kwa namna yake alivyoweza.

Hivi jamani mnaendeshwa kwa spidi kubwa kiasi hiki mnakaa kimya tu, hamjui kama ni hatari kwenu?

Abiria wote tulikaa kimya. Mimi ndo nilikua muoga sana kwani niliamini askari yoyote angeweza kunikamata na kunitia ndani kwa makosa niliyoyafanya.

Yule askari aliongea sana na kutupa somo kuhusu usalama barabarani na mara nikaona anamuandikia cheti yule dereva kumpiga faini. Baada ya kumaliza tuliendelea na safari ambapo tulifika salama Tanga mjini. Sikukawia, haraka haraka nikaenda kukata tiketi na kufanikiwa kupata basi la mwisho kabisa jioni. Kwa kuwa muda wa safari ulikua haujafika, nikaamua kwenda kwa wakala ili nikasajili line mpya ya simu maana niliamini ile line yangu ilikua haifai tena kwa majanga niliyokua nayo. Tangu niondoke Dar simu yangu niliizima na sikuiwasha hadi muda huo. Baada ya kumaliza kusajili line niliiweka kwenye simu na mtu wa kwanza kabisa kumpigia alikua ni Winnie. Simu iliita sana na haikupokelewa na nilirudia tena kupiga. Iliita tena kidogo na nikasikia imepokelewa.

Hello.

Hello, Winnie mambo vipi?

Alex?

Ndio, ndo mimi.

Alex upo wapi?

Sipo Dar Winnie, vipi huko nini kinaendelea?

Huku hali sio nzuri hata kidogo Alex. Hapa ninavyokwambia kesho ninapelekwa hospitali kutoa mimba. Mama amesema ni lazima hii mimba itolewe.

Kwani wewe unaonaje?

Hata sijui Alex nimechanganyikiwa sana. Ila naogopa sana kutoa mimba.

Haina jinsi Winnie inabidi tu ukubali maana wazazi wako hawawezi kukubali kuona unazaa na mimi kama mama yako ulivyomsikia kuwa ni lazima anifunge. Hakuna njia nyengine inabidi tu utoe.

Mhh! naogopa sana.

Usiogope, kila kitu kitakua sawa tu.

Sawa Alex ila naomba kwa sasa usije nyumbani maana mama ana hasira sana na anaweza akakufunga kweli.

Sawa Winnie nimekuelewa.

Tuliongea mambo mengi sana na mwisho nikakata simu.

Kiukweli nilikua na mawazo sana na hata nilikua sijui nikifika Dar nitafanya nini maana hata kwenda nyumbani kwangu nilikua naogopa. Niliwaza sana hadi nilipokuja kushtuliwa na honi ya basi ikiwashtua abiria kuwa muda wa safari ulikua umewadia. Niliinuka na kwenda kwenye basi ambapo baada ya muda mfupi safari ya Dar ilianza.


*************** ***************


Zilipita siku mbili tangu nirudi Dar na niliamua kupanga kwenye hotel ya bei ya chini kidogo ili kupunguza matumizi. Muda wote huo bado nilikua natembea na hela kwenye begi kwani niliona nikienda kuziweka benki na kupata dharura ya ghafla, nitapata tabu sana kwenye kuzitoa kama ujuavyo benki pindi unapotaka kutoa hela nyingi.

Muda mwingi nilikua nakaa ndani tu kwa kuhofia nikitembea naweza nikakamatwa. Ilipita wiki moja nikiwa nipo pale hotelini na nilitamani sana kujua nini kinaendelea kuhusu Winnie, na kama David ameshajua kuhusu wizi nilioufanya. Muda wote huo sikuona simu ya Winnie na nikaanza kuhisi huenda kuna kitu hakipo sawa maana kwa ninavyomjua, ni lazima angenitafuta tu. Ilinibidi nimpigie simu ili kutaka kujua suala la ujauzito limefikia wapi. Nilipigia zaidi ya mara tatu lakini mara zote simu haikupokelewa. Nikaamua kutuma meseji na kumuuliza nini tatizo hadi anashindwa kupokea simu lakini ile meseji haikujibiwa. Niliamua kumuacha na kuhisi huenda labda atakua yupo mbali na simu, na akiwa karibu nayo atanitafuta tu.


Sio siri mawazo yalinitawala sana kiasi kwamba kwa kipindi hiko sikujua nini nifanye. Ilipofika ijumaa niliamua kwenda maeneo yangu ya viwanja nikapunguze mawazo. Begi la hela nililifungia ndani hotelini na nilitoka na funguo kimya kimya bila kuaga. Nilienda kiwanja kimoja maarufu kilichopo maeneo ya Sinza na kukaa peke yangu kwani sikutaka kampani ya mtu yoyote kwa siku hiyo. Nilikunywa sana hiyo siku kiasi kwamba hadi nikaanza kujihisi kama sina mawazo vile.


Wakati bado naendelea kukata maji nilishangaa mtu akija na kunishika bega kisha akakaa kwenye kiti cha pembeni yangu. Nilipomtazama sikuamini nilipomuona Naomi, rafiki yake na Janeth na moyo ulinipasuka sana kwani sikutegemea hata kidogo kumuona mahali pale..........



Hey! mambo.

Poa tu Naomi, habari yako.

Nzuri, za siku nyingi?

Nzuri, kumbe upo hapa?

Ndio ila nimefika muda sio mrefu.

Ooh! sawa. Upo peke yako au?

Niliuliza ili kujua kama Janeth nae yupo eneo lile.

Yaah! nipo peke yangu.

Sawa, karibu.

Nilimkaribisha mezani ili aungane na mimi kuyakata maji. Naomi alionekana kuwa na furaha sana kwani muda wote alikua anatabasamu tu. Nilimuita muhudumu na Naomi aliagiza kinywaji alichohitaji.

Nasikia ulipata mtoto!

Ndio nilibahatika kupata mtoto wa kiume anaitwa Kelvin.

Hongera sana.

Asante sana.

Kwahiyo mtoto anaishi wapi?

Nipo nae na mama yake, wote naishi nao.

Kumbe ulishavuta jiko kabisa, hongera sana.

Naomi aliongea huku akiwa anacheka kwa mzaha.

Hapana bado sijamuoa, tunaishi tu pamoja.

Fanya umuoe mtoto wa watu sio ushamzalisha basi unamtelekeza. Kwanza usiku huu imekuaje mpaka upo hapa wakati una mtu unaishi nae?

Hayupo amesafiri.

Nilimdanganya ili asizidi kuniuliza maswali mengi zaidi ambayo nilishaanza kuyaona kero.


Tuliongea mambo mengi sana huku tukiendelea kukata maji. Siku hiyo nilikua nakunywa kwa uangalifu sana ili nisipoteze fahamu zangu. Naomi alikua hata hajali kwani alikunywa sana hadi akalewa chakari. Ghafla nikaanza kumuona akiniangalia kwa macho ya matamanio sana ya kunishawishi nifanye kitu huku akiwa anazing'ata lips zake. Kwa umri wangu wala sikutaka kuisumbua akili kujua nini anataka kwani mitego ya aina ile nilishakutana nayo mara nyingi sana kwenye maisha yangu. Nilijifanya kama sielewi kitu vile kwani niliendelea kunywa na hata sikua na habari nae. Tulikaa maeneo yale mpaka saa 9 za usiku na Naomi alikua amelewa kiasi kwamba hata kutembea alikua hawezi.

Alex mwenzio nina usingizi.

Sawa, basi tufanye tuondoke ukapumzike. Umekuja na usafiri au?

Ndio nimekuja na gari yangu.

Sasa kwa hali hiyo uliyonayo utaendesha vipi?

Kwani hatuondoki wote.

Naomi aliuliza kwa sauti ya kilevi sana kwani alilewa kupita kiasi.

Kwenda wapi?

Si kupumzika.

Hapana mimi ninarudi nyumbani.

Sasa mimi unaniachaje hapa nipo hivi?

Naomi alizidi kuongea vitu ambavyo vilinichanganya sana.

Kwani unaishi wapi?

Naishi Goba.

Sasa nikikupeleka Goba unazani nitarudi vipi na huu usiku?

Kwani si umeniambia mchumba wako amesafiri? Utalala kwangu mpaka asubuhi, au kuna ubaya?

Aliniuliza huku akiwa ananiangalia usoni na macho yake yamelegea sana.

Hapana Naomi sitaweza kulala kwako maana sijajua kwako kupo vipi na unaishi na nani.

Ina maana Alex hauniamini? Naishi peke yangu na mfanyakazi, watoto wangu wawili wameenda likizo kwa bibi yao Moshi.

Mume wako yuko wapi?

Mbona nilishaachana nae siku nyingi sana. Usiogope bwana hakuna shida yoyote.

Kidogo maneno yake yalinitia moyo na nikajikuta nalegeza kamba bila kutarajia.

Sawa ila kesho mapema sana nitaondoka.

Sawa Alex usijali.


Kweli tukainuka na kutoka kuelekea Naomi alikopaki gari yake. Alinikabidhi funguo na tukaingia mpaka ndani na kuanza safari ambapo alikua akinielekeza njia maana sikuwahi kufika kwake hata mara moja. Baada ya kama nusu saa tulifika salama na akampigia simu mfanyakazi wake wa ndani ambaye alikuja kufungua geti. Niliingiza gari ndani na kushuka.

Yule mfanyakazi alifunga geti na kuja kunisalimia ambapo alionekana kuwa na heshima sana. Tuliongozana mpaka sebuleni ambapo nilikaa kwenye sofa na Naomi alikaa pembeni yangu. Sio siri nyumba yake ilikua nzuri sana na sikupata jibu kama aliijenga yeye mwenyewe au aliachiwa na mume wake wakati wanaachana. Mfanyakazi alirudi chumbani kwake maana alionekana kama mtu aliyetoka usingizini na akatuacha sisi wawili tu.

Alex twende chumbani basi mwenzio nina usingizi.

Chumbani kwako?

Ndio.

Sasa mimi nitalala vipi chumbani kwako?

Alex bwana usijifanye mtoto mdogo, twende bwana.

Alikua anaongea huku macho na sauti amevilegeza sana kiasi kwamba nikawa nishajua nini anataka. Nikamuona anainuka na kunishika mikono akiashiria na mimi niinuke ili twende chumbani. Kiukweli sikua na pingamizi hata kidogo kwani kwa jinsi Naomi alivyojazia, ni wanaume wachache sana ambao wangepata ujasiri wa kumkatalia haswa kwa mazingira kama yale tuliyokua. Nikainuka na tukaongozana mpaka chumbani kwake ambapo palikua ni pazuri sana utadhani ni hotel ya nyota tano. Akaanza kuvua viatu vyake virefu alivyovaa kisha akamalizia na kigauni chake chekundu kilichokua kinaishia mapajani. Alibaki na kufuli na sidiria tu kitu kilichoamsha vilivyo hisia zangu. Akanisogelea kunikalia mapajani na kuanza kunichezea chezea kifua changu huku taratibu akianza kunifungua vifungo cha shati langu. Naomi hakua na aibu hata kidogo na nikajua ni zile pombe nyingi alizokunywa ndo zilimtoa aibu yote. Baada ya kumaliza tukaanza kubadilishana mate taratibu huku akiwa ananishika shika maeneo ya kwenye bunduki yangu ambayo taratibu ilianza kutii sheria na kujikoki tayari kwa mashambulizi. Baada ya hapo tuliachiana na Naomi akaanza kunivua suruali ambapo nilimsaidia na kuitoa yote. Nikamalizia kuitoa boxer niliyovaa na kubaki mtupu kama nilivyokuja duniani. Akaikamata dunguso na hata hakuchelewa akaanza kutuma salamu kwa ndugu, jamaa na marafiki ambapo nilianza kusikia raha za hali ya juu. Naomi alijua kuitendea haki dunguso yangu na nikazidi kuamini kuwa kazi za wanawake, wasichana hawaziwezi kwani nilimfananisha kabisa na Janeth kwa ufundi wao wa kutuma salamu. Bwana mkubwa alikua amesimama barabara kama msitimu na alikua na hasira za kufa mtu. Baada ya kumaliza fujo zake zote, aliniachia uwanja wa fundi seremala ambapo nikaanza kuutawala mchezo. Nilianza kumnyonya masikioni hadi shingoni ambapo alianza kutoa sauti laini sana. Nikaanza kushuka taratibu hadi maeneo ya kifuani na kuanza kuyanyonya matiti yake makubwa yaliyojazia na kuzivuta chuchu zake ambapo alifumba macho kuashiria anapata raha za hali ya juu. Niliendelea na ule mchezo kwa muda na taratibu nikazidi kushuka chini hadi kwenye kitovu chake kilichoingia kwa ndani na kuanza kuupitisha ulimi wangu ambapo alizidi kupagawa. Balaa lilizidi kuwa kubwa nilipohamia kunako chumvini kufanya vitu vyangu ambapo Naomi ndo alikua kama anaamka kutoka usingizini kwani alikua anapiga kelele sana na nikajua tu mashetani yake yote yamelala huko. Nami sikutaka kupoteza CV yangu kwani niliuzungusha vilivyo ulimi wangu hadi akawa ananishika kichwani akinizuia nisitoke maeneo hayo. Nilimpagawisha sana hadi akawa ananiomba nianze kazi na kweli sikumchelewesha, kwani haraka nilimpeleka bwana mkubwa kwenye pango la Amboni aende kutalii. Naomi alimsikia barabara wakati anaingia kwani alitoa sauti laini sana na kufumba macho huku akiwa anang'ata lips zake. Nilianza kumpelekea moto wa hatari na hazikupita hata dakika mbili akaandika goli la kuongoza. Alipiga kelele sana na sikumuacha apumzike kwani niliendelea na dozi yangu ya mwana ukome na baada ya muda mfupi akaandika tena goli jengine. Nikahisi huenda Naomi huwa hakutani na wanaume mara kwa mara kwani alionekana ny*g* zilikua zimemjaa sana. Siku ile nilimpa raha sana Naomi kiasi kwamba pombe zote zilimtoka na akawa analia sana hadi machozi yakawa yanamtoka. Baada ya safari ndefu hatimaye na mimi nilifika mwisho wa reli na kufunga breki ambapo nilikua nahema sana kwa ile shughuli nzito niliyotoka kuifanya ya kumridhisha mtu mzima aliyejazia kama Naomi.


Tulikaa kimya kwa muda na nilipomtazama Naomi nilimuona akiwa amefumba macho huku mdomo akiwa ameuacha wazi. Niliendelea kumtazama na nikajiona sina maana hata kidogo kwa kitendo cha kutembea hadi na rafiki wa damu wa Janeth. Naomi aligeuka na kuniangalia huku akinishika ndevu zangu.

Asante sana Alex, leo ndo nimeelewa kwanini Janeth amechanganyikiwa kiasi kile juu yako. Mambo unayaweza.

Nilibaki natabasamu tu na bichwa kuvimba kwani sisi wanaume huwa tunajivunia sana pindi unapompa dozi mwanamke na akakubali kweli umejua kumfikisha pale anapopataka.

Mwanamke wako anafaidi sana Alex.

Kwanini?

Si hizi raha unazokua unampa kila siku.

Nilibaki nacheka tu kwani nilishazoea kuambiwa maneno kama yale na wanawake wengi niliokutana nao. Baada ya muda mfupi nikaanza kuhisi bwana mkubwa anaamka tena kutoka usingizini na hatukuchelewa kwani tuliendelea tena na mchezo na usiku huo tulipelekeshana sana, kwani na yeye alijua kunipagawisha.


*************** ***************


Kesho yake mida kama ya saa nne asubuhi nilirudi hotelini nilikopanga na wakati naanza kupandisha ngazi kuelekea juu kilipo chumba changu nikasikia mtu ananiita. Niligeuka na kumuona muhudumu wa kike ambaye niliikumbuka sura yake.

Habari yako kaka.

Nzuri tu, mambo vipi.

Poa. Vipi mbona jana haukurudi na funguo ya chumba chako haionekani?

Ooh! samahani sana, kuna sehemu nilienda nikalala huko huko na wakati natoka nilikua na haraka sana hivyo nilijisahau kabisa kuacha funguo.

Sawa, ila muda mwengine usirudie tena maana si ruhusa kwa mteja kuondoka na funguo.

Sawa dada yangu, poleni sana kwa usumbufu wowote uliojitokeza.

Sawa kaka usijali. Nakuja muda sio mrefu kufanya usafi huko.

Sawa dada usijali nitakupisha.

Nilimaliza kuongea naye na kupanda ngazi hadi juu chumbani kwangu. Niliondoka na funguo makusudi ili mtu yoyote asije kuingia mule na kuanza kupekua maana pesa zangu nilizomuibia David niliziacha mule. Niliingia na kwenda kuziangalia na nikakuta zipo kama nilivyoziacha. Nikakaa kitandani na kuanza kutafakari ni kitu gani nifanye maana sikutaka kuondoka na kumuacha mtoto wangu nyuma ukizingatia bado alikua mdogo sana. Baada ya kufikiria kwa muda mrefu nikajikuta napata wazo la kuiuza nyumba yangu na kuhamia mkoani pamoja na Vee na mtoto wetu maana nilishaona Dar sio sehemu salama tena kwangu.


Wakati naendelea kuwaza na kupanga mipango ni jinsi gani nijinasue na ule mtihani niliokua nao, nilisikia mlango wa chumba changu ukiwa unagongwa. Nilishtuka sana na nikaanza kujiuliza itakua ni nani maana kwa majanga niliyokua nayo, nilikua naogopa kila mahali ninapokaa.............



Nikainuka taratibu na kwenda kuzificha pesa kabatini na kufunga na funguo kisha nikaanza kutembea taratibu kuelekea mlangoni. Niliitia funguo ya kabati mfukoni kisha nikafungua mlango kwa wasiwasi sana ambapo nilikutana uso kwa uso na yule dada muhudumu.

Vipi ulikua umelala nini?

Hapana, nilikua chooni.

Sawa, ndo nimekuja kufanya usafi.

Sawa karibu.

Nilimkaribisha kisha nikaenda kuchukua simu yangu na kumpisha mule chumbani ambapo nilishuka chini na kwenda kwenye mgahawa kupata kifungua kinywa. Nilipata kifungua kinywa huku nikiwa naangalia TV iliyokuwepo mahali pale na nilikuja kushtuka sana nusu nipaliwe na chai pindi nilipoona taarifa ya habari kwenye kituo kimoja cha TV ikiwa inanizungumzia mimi kuwa ninatafutwa kwa kosa la mauaji na zawadi nono sana itatolewa kwa yeyote atakayefanikisha kupatikana kwangu. Sikujua hata niliinuka vipi pale kwani nilichowaza ni kwenda chumbani kubeba begi langu la nguo na hela kisha niondoke. Nilifika mpaka juu chumbani na kumkuta yule dada bado anafanya usafi.

Vipi kaka bado sijamaliza.

Naomba nichukue mizigo yangu naondoka.

Unaondoka? mbona ghafla kiasi hiki?

Nimepata dharura inabidi niondoke muda huu.

Nikajikuta naanza kumuhisi vibaya yule dada kwa ameshajua kuwa natafutwa maana alikua kama ana wasiwasi na mimi hivi. Nikaelekea kabatini na kufungua kisha nikatoa mizigo yangu. Nilipogeuka nyuma nikaona yule dada akiwa ameshika kisu mkononi na kunitazama huku akiwa amekunja sura sio kawaida.


Hauwezi kutoka hapa nimeshakujua wewe ndo muuaji unayetafutwa.

Nilimtazama kwa macho yaliyojaa roho mbaya sana na kuanza kupiga mahesabu namvamia vipi ili niweze kutoka pale.

Dada yangu naomba usijitafutie matatizo ukaisononesha familia yako. Naomba unipishe niondoke.

Hauwezi ukatoka hapa na tayari nimeshawapigia simu polisi wapo njiani. Siwezi nikaacha hiyo zawadi nono inipite hivi hivi.

Nikaona sasa kweli yupo serious na hatanii hata kidogo. Niliingiwa na ujasiri wa hali ya juu kwani nilimtupia begi langu la nguo huku nikiwa namkimbilia ambapo alivyolikwepa nikapata nafasi ya kumshika na kuanza kumpokonya kisu ambacho kilionekana kuwa kikali sana. Akaanza kupiga kelele lakini nilimzuia kwa kumziba mdomo huku nikizidi kumdhibiti na kufanikiwa kumpokonya kisu.

Nataka unyamaze kimya bila hivyo nakumwaga utumbo sasa hivi hapa.

Alibaki anatetemeka sana na kweli alikaa kimya.

Chukua zile kamba pale juu ya kabati na ujifunge mikononi.

Nikaona anasua sua na ilibidi nimkaripie kwa sauti ya juu kidogo ambapo aliichukua kamba na kuanza kujifunga nilipoona amejizungushia mikononi kote nilimsogelea na kuzikaza vizuri kisha nyengine nikamfunga miguuni. Nilipomaliza nilichukua taulo na kumuingiza nalo mdomoni ili asipige kelele.

Usipende kuwa kimbelembele kwa tamaa zako utaishia pabaya sana malaya wewe.

Niliongea kwa dharau kisha nikabeba mizigo yangu haraka na kuanza kuondoka. Nilimfungia mlango kwa nje kisha nikatoka hadi mapokezi. Nilikabidhi funguo na kusaini kisha nikaanza kuondoka ambapo niliona dada aliyekua mapokezi akiniangalia sana. Sikutaka kugeuka nyuma kwani nilizidisha mwendo haraka na kwenda hadi kituo cha tax. Niliita tax na haraka nikaingia ndani na mizigo yangu na kumuelekeza dereva anipeleke Mbezi nyumbani kwangu maana nilishaona maisha ya kukaa hotelini sio salama tena. Wakati ndo tunaanza kuondoka kama dakika moja tu, tulipishana na gari mbili za polisi na nikajua moja kwa moja itakua zimekuja kunikamata mimi tu. Nilimsihi dereva aongeze mwendo kwa kujifanya nina haraka kumbe lengo langu lilikua ni kuwakimbia polisi. Kweli dereva aliongeza mwendo na kwa mida hiyo ya saa 5 asubuhi foleni za Dar huwa sio kubwa, tulifika haraka sana nyumbani kwangu na nikamlipa dereva pesa yake. Nilishusha mabegi yangu na kuingia ndani haraka haraka ambapo nilimkuta mfanyakazi akiwa yupo na mtoto wangu. Kiukweli kwa misukosuko niliyokua napitia, nilijikuta nikiwa nimemkumbuka sana mwanangu Kelvin na haraka nikaweka mabegi yangu chini na kwenda kumuinua na kumbeba.

Shikamoo shemeji.

Marahaba haujambo?

Sijambo.

Vipi habari za hapa.

Nzuri tu shemeji.

Dada yako yupo wapi?

Ametoka tangu asubuhi ila hakuniambia anapoenda.

Sawa. Hakuna mtu yoyote aliyekuja kuniulizia?

Hapana sijamuona mtu yoyote.

Sawa. Nisaidie kunibebea mabegi yangu niletee chumbani.

Nilimwambia huku nikianza kuelekea chumbani nikiwa nimembeba mtoto wangu. Aliniletea mizigo mpaka chumbani na kutoka na nikabaki na Kelvin tu nikiwa nacheza nae. Nilibaki najiuliza kama pale nyumbani watakua wameshapata taarifa juu ya mauaji niliyoyafanya na nikabaki bila jibu. Nikaamua kumtumia meseji Vanessa na kumtaarifu kuwa nipo nyumbani kwa kupitia ile namba yangu mpya ambayo alikua haijui. Muda huo huo akanijibu kuwa yupo njiani na atafika muda sio mrefu. Nikabaki na mawazo sana na kujiuliza nianzie wapi kutafuta wateja wa kuinunua nyumba yangu kwa haraka ili tuhame pale maana sura yangu ilishaanza kuwa maarufu miongoni mwa baadhi ya watu hivyo niliogopa hata kutembea.


Nilikaa takribani nusu saa na zaidi ndipo nilipomuona Vee akifungua mlango wa chumbani kwa haraka sana na kunikimbilia kuja kunikumbatia. Ghafla nikamuona akianza kulia na nikaanza kuhisi huenda itakua ameshajua kila kitu.

Mume wangu ulikua wapi?

Aliongea huku akiwa analia.

Matatizo mke wangu, nipo kwenye matatizo makubwa sana.

Vee alizidisha kulia hadi nikahisi kuchanganyikiwa na ilibidi tuache kukumbatiana na nikamtazama usoni.

Vee mbona hivyo unalia sana?

Why did you kill that man? ( Kwanini ulimuua yule mtu?)

Ndo nikajua rasmi sasa kwamba Vanessa anajua kila kitu kwani nilishatangazwa mpaka kwenye habari.

I'm sorry, i'm so sorry! (Samahani, samahani sana!)

He was innocent, why did you take his life? (Alikua hana hatia, kwanini umeyachukua maisha yake?)

Nilihisi kama Vee anashindilia msumari wa moto kwenye kidonda changu kwani kwa matatizo niliyokua napitia, nilishaanza kujuta kwa unyama wote nilioufanya.

Mapenzi. Nimefanya yote hayo kwa sababu ya mapenzi mke wangu.

Nikajikuta taratibu na mimi machozi yanaanza kunitoka.

Yuko wapi sasa huyo Agness? Umempata?

Vee just stop, please just stop. (Vee nyamaza, tafadhali nyamaza)

Yale maneno aliyoniambia yaliniumiza sana na kunifanya nizidi kujuta kwani hata nilivyotegemea kama kumuua Shaffih ndo ningeweza kumrudisha Aggy haikua kweli.

Tazama sasa unavyoishi kama panya, umeharibu maisha yako. Umeharibu maisha yetu Alex. Hivi unadhani ukikamatwa unatuacha vipi huku mimi na Kelvin?

Nilizidi kulia maradufu na kujuta sana kwa nilichokifanya.

Nakuhitaji sana Vee kuliko wakati wowote ule kwenye maisha yangu. Naomba usimame na mimi maana sina tena mtu mwengine ninayemtegemea.

Alex mimi nitafanya nini sasa, nitafanya nini mimi?

Inabidi tuuze hii nyumba na tuondoke Dar es salaam haraka iwezekanavyo. Wewe ndo inabidi usimame kwa kila kitu maana mimi siwezi tena kuhangaikia hilo kwa jinsi ninavyotafutwa.

Alex yani tuuze nyumba yetu kweli?

Haina jinsi Vee, inabidi tuiuze tu na tukaanze maisha mapya mkoa wa mbali sana na hapa. Dar sio sehemu salama tena kwangu na sipo tayari kuona naishia gerezani na kuwaacha nyie huku peke yenu.

Vanessa alianza kulia tena na ilibidi nimsogeze kifuani na kumkumbatia.

I'm so sorry my love. You don't deserve to go through all these. (Samahani sana mpenzi wangu, haustahili kupitia yote haya)

Vanessa hakujibu kitu na alizidi kulia.


Nilimbembeleza sana hadi mwisho akanyamaza.

How do we get started? (Tunaanza vipi?) Mimi sijui chochote kuhusu mambo ya kuuza nyumba.

Vee aliongea kwa unyonge sana hadi nikamuonea huruma.

Nenda pale Mbezi mwisho kwenye ile bar tuliyoenda ile mkesha wa mwaka mpya kuna madalali wengi sana wakubwa wanaoweza kulifanikisha hili jambo kwa haraka. Kuhusu bei inabidi tuuze hata kwa hasara tu ili tuhame haraka. Waanzie milioni 50 ila isishuke milioni 35. Naamini tukiipata hiyo ukijumlisha na pesa nilizokua nazo kwenye akaunti. Pia hapa ndani nina kama milioni kumi hivi hivyo zote hizo zitatusaidia sana kwenda kuanza maisha mapya.

Sawa mume wangu nimekuelewa na nakuahidi nitakua na wewe bega kwa bega. I know you are not a bad guy, (Najua wewe sio mtu mbaya) ila umefanya yote hayo kwa ajili ya mapenzi tu. Nitasimama na wewe mpaka dakika ya mwisho kwa lolote litakalotokea.

Kiukweli sikua hata neno lenye kufaa au kumtosha Vee kwa wakati huo kwani aliugusa sana moyo wangu kwa maneno yake. Nilimsogelea na kumbusu kwenye paji lake la uso.

If we get passed through this, when the storm is over, i promise i'll marry you. (Kama tutavuka hili, pale kimbunga kitakapoisha, nakuahidi nitakuoa.)

What? are you serious? (Nini? upo makini?)

I'm serious babe. (Nipo serious babe)

Vee alinisogelea na kunikumbatia huku machozi yakiwa yanamtoka.


**************** ****************


Kweli Vee aliwaleta madalali nyumbani na walipoithaminisha nyumba walikubali kweli bei ya shilingi milioni 40 pamoja na samani zote za ndani ni halali kabisa na watapata faida kubwa sana kwani wao wanaweza kuuza hata kwa milioni 50 au zaidi. Nyumba yetu bado ilikua mpya na nzuri sana ila matatizo tu ndo yalitulazimisha tuiuze. Walipiga picha sehemu zote za muhimu na kubadilishana namba za simu kisha wakaondoka na kutuahidi kuwa watakuwa wanatupa mrejesho mara kwa mara.

Baby hivi unadhani tukihama hapa tutaenda kuishi wapi?

Vee aliniuliza wakati tupo chumbani tunapanga mipango yetu.

Nafikiri itakua vizuri tukienda kuishi sehemu ya mbali lakini yenye mzunguko mzuri wa hela kama Mbeya au Mwanza.

Kweli eeh?

Ndio, tena nafikiri Mwanza ndo kuzuri zaidi.

Sawa mume wangu.

Vee alienda jikoni kuandaa chakula na aliniacha peke yangu nikiwa bado nawaza na kuwazua.


Kusema ukweli nilitamani sana kujua nini kinaendelea kwenye familia ya David haswa Winfrida maana alikua ana ujauzito wangu. Nilipiga moyo konde na kuamua kuandika namba yake na kumpigia ambapo niliposikia simu inaita nilihisi moyo ukienda mbio sana.......


Simu iliita mpaka ikakata lakini haikupokelewa na nikawa najiuliza kama Winnie anafanya makusudi kutopokea au yupo mbali na simu maana hata simu yenyewe huwa anaitumia kwa kujificha sana pindi anapokua nyumbani kwao. Nilijiuliza kama dakika mbili nikaamua nimpigie tena ambapo safari hii iliita kidogo tu ikapokelewa na kuisikia sauti ambayo niliitambua vizuri kuwa ni Winnie.

Hallo.

Winnie, mambo vipi?

Alex! vipi upo wapi? (Kwa mshangao)

Nipo Winnie, vipi hali yako?

Nzuri tu, sijui wewe.

Mimi matatizo tu yameniandama.

Nilivyomaliza kusema hivyo tu ghafla nikasikia simu imekatika na nikabaki najiuliza nini tatizo maana kama ni salio lilikuwepo la kutosha. Wakati bado najiuliza nikaona Winnie akinipigia na nilipokea haraka.

Eeh vipi Winnie?

Sorry (Samahani) kuna kitu nilikua naweka sawa.

Sawa usijali, vipi umefikia wapi kuhusu suala la mimba?

Bado ninayo na tayari baba ameshajua.

Unasemaje?

Ndio, kuna matatizo mengi sana ila siwezi kukuambia kila kitu kwenye simu hivyo naomba tukutane.

Mhh lakini si unajua kama kukutana mimi na wewe ni hatari sana kwa kipindi hiki?

Ndio nafahamu ila tutakutana sehemu iliyojificha sana ili tusionekane na mtu yoyote.

Kama ndo hivyo sawa, niambie tukutane wapi.

Nafikiri maeneo ya Coco Beach itakua vizuri sana.

Basi sawa, tufanye kesho mchana.

Sawa nikiwa natoka nyumbani nitakupigia simu.

Sawa Winnie nimekuelewa.


Tulimaliza kuongea na kuelewana vizuri sana. Nikahisi huenda bado David hajashtuka kama nimemuibia pesa maana Winnie hakunigusia chochote kuhusu hilo wakati ni jambo kubwa sana. Muda huo kichwa kilijaa mawazo sana kiasi kwamba sikuwa na hamu ya kufanya kitu chochote kwa muda huo.Vee alikuja kuniita nikale chakula na ilibidi niende tu nikale ili nimfurahishe lakini sikua na hamu ya kula hata kidogo.


**************** ****************


Kesho yake kama nilivyokubaliana na Winnie, mida ya saa 8 mchana nilitoka nikiwa nimevalia shati jeusi, jeans ya blue, kofia nyeusi na miwani nyeusi. Nilikodi bajaj mpaka maeneo ya Coco beach ambapo nilimlipa mwenye bajaj na kutafuta sehemu yenye kivuli na kupumzika maana jua lilikua linawaka sana. Nilimpigia simu Winnie ambaye alinijibu kuwa ameshakaribia kufika yupo kwenye bodaboda. Niliendelea kumsubiri na baada ya muda wa kama robo saa nikaona akiwa ananipigia simu akinielekeza mahali alipo. Tulielekezana na baada ya muda mfupi nikamuona akiwa anakuja mahali nilipo.

Winnie alionekana kuwa mnyonge sana na alikuja kukaa pembeni yangu.

Mambo vipi Winnie.

Poa, za kupotea.

Bwana, we acha tu majanga juu ya majanga.

Winnie aliguna tu bila kuongea kitu chochote.

Jana uliniambia kuwa tayari baba yako anajua kila kitu, vipi mlimwambia au?

Ndio, alianza kuhisi kama kuna tatizo na baada ya kutaka kujua kweli ilibidi mama amwambie tu maana ni lazima angekuja kujua. Mwanzo nilikua namdanganya kuwa nimerudi kutoka shule kwa sababu ninaumwa ila kadri siku zilivyozidi kwenda ndo alivyokuja kushtukia mchezo.

Umemwambie kama mimi ndiye niliyekupa mimba?

Dada Happy amemwambia kila kitu na kumbe baba alikua ameshajua kuhusu mahusiano yako na dada ila alichukulia kawaida tu kwani aliona sio kitu kibaya sana.

Wee usiniambie, kumbe alikua anajua?

Ndio, ila baada ya kujua kama umenipa mimba ndo amekasirika sana na ameapa lazima akutie mikononi akufanye kitu chochote kibaya.

Ile kauli ya Winnie ilininyong'onyesha ghafla na kujikuta nakuwa mpole.

Sasa hivi yupo hapa Dar au amesafiri?

Yupo hapa hapa.

Daah! kwahiyo kuhusu hiyo mimba wazazi wako wana mpango gani?

Mama anataka ikatolewe lakini baba hataki anasema Mungu hapendi kabisa hivyo vitu basi hapa nimebaki njia panda sijui nini nifanye.

Vipi wewe mwenyewe, nini msimamo wako?

I don't know. (Sijui) Hata sijui kwakweli nimechanganyikiwa sana.

Nilibaki kimya nikiwa natafakari nini cha kumwambia ili angalau nimpe mwanga ajue nini cha kufanya.


Tuliongea sana huku nikiwa namfariji sana Winnie na kumpa moyo kuwa asikate tamaa kila kitu kitakua sawa. Wakati bado tunaendelea kuongea, niliona gari nyeusi aina ya Noah Voxy ikipaki nyuma yetu kwa mbali kidogo huku ikiwa imewekwa vioo vya tinted mpaka juu. Nilikua naongea huku nikiitazama na baada ya kuona hakuna mtu anayeshuka kutoka kwenye ile gari, nikajikuta naachana nayo na kuendelea na maongezi na Winnie.

Alex nahisi siku za hatari sana mbele yetu na sijui kama tutapata bahati ya kuonana tena mimi na wewe baada ya siku hii ya leo.

Kwanini unasema hivyo Winnie?

Nauona mwisho wetu umeshafika.

Mhh! ujue bado unaniweka njia panda, una maana gani unaposema hivyo?

Winnie alikaa kimya kwa muda akiwa ameinama chini na nikawa nasubiri ataongea kitu gani maana aliniweka njia panda kwa maneno yake.


Wakati bado namuangalia Winnie, nilishtuka kuona jamaa wawili wenye miili iliyojazia wakiwa wamesimama mbele yangu. Nilishtuka sana maana kwa majanga niliyokua nayo, nilijua kivyovyote vile watakua wamenifuata mimi tu. Niliinuka na kuangalia namna ya kujitetea ila nilipogeuka nyuma na kutaka kukimbia niliona vijibaba wengine wawili wa miraba saba na ghafla nikajikuta nakua mpole.

I'm sorry Alex, i had no choice, (Samahani Alex, sikua na chaguo) baba ndo aliyenilazimisha kufanya yote haya. Pia kuhusu mimba tayari nilishatolewa hii wiki ya tatu sasa na niliumwa sana kidogo nipoteze maisha. Alex wewe ni mtu mbaya sana ambaye wakati unakuja nyumbani ulijivalisha ngozi ya chui kumbe ni kondoo. Kwa taarifa yako wote tunajua kila kitu mpaka mauaji uliyoyafanya.

Winnie, kwanini unanifanyia hivi lakini? Ina maana...

Sikumaliza hata kuongea nikashtukia wale majamaa wakinichota na kunibeba juu juu na kuanza kuondoka na mimi.

Jamaniiii, nisaidieniii....Nakufaaa, Hawa watu wanataka kuniua mimi..Nisaidieniiiii.

Kiukweli nilipiga kila aina la yowe lakini sikuona hata mtu mmoja aliyejaribu kusogea japokua palikua na watu wengi kiasi. Haraka haraka nikaona naingizwa kwenye ile Noah nyeusi niliyoiona wakati inakuja na mlango ulifungwa kwa haraka sana na Winnie nikamuona akiwa anaondoka peke yake. Kwa mwendo wa haraka sana gari ilianza kuondoka huku nikivalishwa kofia kubwa aina ya mzula na kufunika uso wangu wote kiasi kwamba sikuona kitu chochote.

Jamani mnanipeleka wapi ndugu zangu? Tafadhali naomba msinifanye kitu chochote kibaya.

Tulia malaya wewe. Si unajiona rijali sana na kidume kuliko wanaume wote duniani? Ngoja tukuonyeshe sasa.

Hapana jamani, hapana ndugu zangu msinifanyie hivyo.

Nilikua naongea kwa tabu sana maana ule mzula uliniziba mpaka mdomo.

Kelelee kenge wewe, ghafla nikasikia kitu kikifunguliwa na kukatwa na ghafla wakaupandisha kidogo mzula na kuniweka gundi aina ya sole tape mdomoni na kunifanya nishindwe kuongea kabisa.

Baada ya hapo ukimya ulitawala na gari ilizidi kutembea kwa kasi na baada ya mwendo wa kama nusu saa au dakika arobaini, niliisikia gari ikisimama na geti likifunguliwa. Nikawa najiuliza watakua wamenileta wapi maana yale maeneo yalionekana kuwa tulivu sana. Nilijitahidi kupiga kelele kutaka kuomba msaada lakini sidhani kama sauti yangu iliweza kutoka hata nje ya ile gari tu. Tuliingia mpaka ndani na geti likafungwa kisha mlango wa gari ulifunguliwa na nikateremshwa kwa kubebwa juu juu. Nilijitahidi kufurukuta huku na huko kujaribu kama ningeweza kujiokoa, lakini kwa nguvu walizokua nazo wale jamaa sikuweza kufanya kitu chochote. Nikawa najiuliza hapo waliponileta ni wapi na walikua wanataka kunifanya kitu gani. Waliniingiza ndani ambapo kwa kukisia ilikua ni kama nyumba ya mtu hivi kwa jinsi milango ilivyokua ikifunguliwa. Nilipelekwa mpaka kwenye chumba ambacho nilihisi kama hakina kitu chochote kwani watu wakiongea nilisikia mwangwi ukitokea kwa mbali. Nilikalishwa kwenye kiti na kufungwa kamba barabara mikononi na miguuni kisha wakamalizia na kiunoni. Sikuweza hata kutikisika kwani kamba zilikazwa sana kiasi kwamba zilianza kuniletea maumivu. Wakanivua mzula na kuziona zile njemba nne zikiwa zimesimama mbele yangu zikinitazama. Mawazo yangu moja kwa moja yakajua kuwa zinataka zinifanyie mchezo mchafu wa kuniingilia kinyume na maumbile maana story za aina ile nilishazisikia mara nyingi sana kwa watu. Asikwambie mtu suala la kutekwa baki kulisikia kwa mwenzio tu kwani ni jambo gumu sana kwa mwanadamu kulivumilia maana watekaji huwa na nguvu ya kukufanya kitu chochote wanachotaka. Nilijawa na hofu sana kiasi kwamba hadi jasho likawa linanimwagika wakati hiko chumba kilikua na hewa nzuri sana ya A.C ikipuliza. Baada ya kama dakika tatu niliona jamaa mmoja kati ya wale wanne akiondoka na wakabaki watatu pale. Walikaa kimya bila kuniongelesha kitu chochote na muda wote walikua wakinitazama tu. Muda huo hofu yangu kubwa kuliko zote ilikua ni kulawitiwa tu kwani kila nilivyokua nikivuta picha jinsi zile njemba zitakavyokua zinaufanya mwili wangu kama kahaba wa Kimboka Buguruni, nilijikuta nikiishiwa nguvu kabisa. Baada ya kama dakika 10 hivi na kidogo niliona yule jamaa mmoja kati ya wale wanne akirudi na kuwapa ishara wenzake watoke mule chumbani na kweli wote wanne walitoka na kuniacha peke yangu. Hofu ilizidi kutawala na kujiuliza wanataka kufanya kitu gani maana mpaka muda huo hawakusema kitu chochote.

Ghafla nilianza kusikia mtu akiwa anatembea kwa mwendo wa taratibu na viatu vyake vikitoa mlio kama wa mtu aliyevaa skuna. Nilimsubiri kwa hamu kutaka kujua ni nani na anataka kunifanya nini maana hadi muda huo nilikua na hofu sana. Sikuamini pindi alipotokeza mlangoni na kuingia mule chumbani, kwani alikua ni David akiwa amevalia suti nyeusi na viatu vya skuna kama nilivyodhani.

Habari yako Alex.


Kiukweli nilihisi haja ndogo ikiwa imechanganyika na haja kubwa huku tumbo likianza kunikoroga ghafla na jasho kuzidi kutiririka. Nikajiuliza atakua amedhamiria kunifanya kitu gani mpaka akaniteka na kunipeleka mazingira kama yale.........



Nilimuangalia David kwa uoga sana hadi nikaanza kutetemeka. David alisimama mbele yangu na kuanza kunitazama huku mkononi akiwa ameshika bahasha kubwa kidogo ambayo ilionekana ndani yake kuna kitu.

Alex! Alex Alex! Alex mdogo wangu niliyekutoa kijijini, niliyekutoa kwenye maisha magumu yasiyo na uhakika na kesho yako, niliyekuokoa usipoteze maisha pindi ulipopata ajali na kubaki bila msaada. Nimekuleta mjini na kukaa na wewe nyumbani kwangu kwa moyo mmoja, kwa upendo mkubwa sana kama mdogo wangu wa damu kabisa. Wazazi wako wakawa wazazi wangu, ndugu zako wakawa ndugu zangu, msiba wa baba yako niliubeba kama wa baba yangu na kila kitu kwako nilikifanya kama ndugu yangu wa damu kabisa. Nilikukutanisha na familia yangu na familia yangu ikakupenda sana. Nikakupatia na kazi, nikakufundisha jinsi ya kutafuta pesa na Alex ukaanza kushika pesa. Nikafanikiwa kubadilisha maisha yako hadi ukawajengea wazazi wako nyumba nzuri ya kuishi. Alex ukaanza kupendeza na kuheshimika mpaka ukapata marafiki wenye hadhi na maisha mazuri. Ukaniomba kuhama nyumbani kwangu ili ukaishi peke yako lakini hata sikua na pingamizi kwani siku zote nilitaka nikuone ukisimama vizuri peke yako na kuanzisha familia yako. Ukanitaarifu kuwa unaanzisha ujenzi wa nyumba yako mwenyewe Mbezi na nilikupa kila aina ya msaada ambao ningeweza kuutoa, kuanzia msaada wa kimawazo mpaka pesa. Nilikuongeza mpaka pesa ninayokulipa ilimradi tu ulikamilishe jambo lako kwa wakati na kweli hilo likatimia na ukahamia huko. Alex wa leo sio tena yule Alex wa jana mwenye kuvaa nguo za kupauka na zilizochanika. Alex wa leo anatamaniwa na kila aina ya mwanamke anayehitaji mwanaume bora. Nilikupa kila aina ya uhuru wa mali zangu na kuendesha gari langu lolote ulilotaka na ikafika kipindi hadi nikakuachia ile Mark X japo sikuwahi kukutamkia mdomoni kwa sababu nilijua inakusaidia kwenye mizunguko yako na hata kurahisisha biashara zangu pia. Nilikupa kila kitu Alex ambacho kilikua ndani ya uwezo wangu. Nilikuja mpaka kugundua kuwa una mahusiano na mtoto wangu kipenzi Happy lakini hata siku moja sikuwahi kukuuliza au kukwambia kitu cha aina yoyote kwa sababu nilikuamini na niliamini mnaweza kuja kufika mbali. Happy sio mtu wa kupenda wanaume hivyo hadi nilivyoona amekupenda wewe niliamini kuwa kuna kitu kizuri amekiona ndani yako na siku zote napenda kumuona binti yangu akiwa na furaha. Nilijua kila kitu Alex japo wewe ulidhani hakuna ninachofahamu.


Muda wote huo nilikua nipo kimya na kubaki na bumbuwazi la aina yake kwani sikutarajia kama David alikua anajua yote hayo. Nilikua nikimsikiliza huku nikiwa na hofu sana ni kitu gani anataka afanye kwangu.

Wiki kadhaa zilizopita nilikuaga kuwa naenda Nairobi kikazi na ukafikiri kweli nimeenda Nairobi lakini ukweli ni kwamba nilikua nipo hapa hapa Dar. Nilishaanza kukutilia shaka na ilibidi nipate muda mzuri wa kujua ukweli wa kile nilichokihisi na kuambiwa maana sikutaka kukurupuka kwa kitu nisichokua na ushahidi nacho. Niliajiri vijana watatu kwa ajili ya kufuatilia kila aina ya nyendo yako kwa kila siku na nashukuru wale vijana waliweza kuifanya kazi yao vizuri sana.

Alex! Alex!

Ghafla nikamuona David akianza kubadilika na kuwa kama mtu anayetaka kulia.

Nilivyorudi nyumbani nikakutana na habari nyengine mpya kabisa kuwa mwanangu Winfrida ana mimba na amefukuzwa shule na baada ya kumlazimisha sana aniambie ukweli, dada yake Happy akaniambia kuwa wewe ndo uliyempa hiyo mimba na ndo maana akawa anaogopa kuniambia. Unathubutu kutembea na watoto wangu wote Alex hadi mmoja unampa mimba. Kweli Alex!!? Hivi wewe ni binadamu wa aina gani uliyekosa aibu na busara kiasi hiki? Ona sasa binti yangu umemfukuzisha shule na hapa sijui atakubaliwa wapi kwengine.


Pamoja na kukutendea wema wote huo Alex, haya ndo malipo yake? Haya ndo malipo ninayostahili kuyapata Alex!!?

David aliongea huku akinionyesha ile bahasha aliyoishika mkononi na kuanza kutoa kilichokuwepo ndani yake.

Alex wewe ni wa kunifanyia hivi kweli? Alex!!? Watoto wangu pia umeona hawakutoshi ukaamua kuhamia kwa mke wangu!! Kwanini Alex!!? Nani aliyekutuma uje kuniumiza kiasi hiki?

Aliongea huku akilia kwa uchungu sana na kuzitoa picha nyingi sana na kunirushia ambapo nyengine zilitua kwenye mapaja yangu na nyengine zilidondoka chini. Aisee nilipoziona zile picha siwezi hata kuelezea ni hali gani niliyoipata kwani sikutegemea kabisa kama David alishashtuka kuwa nilikua ninamuibia mke wake. Zilikua ni picha tulizopigwa nikiwa naingia na kutoka hotelini nikiwa nimeongozana na Janeth huku nyengine tukiwa tupo ufukweni tunajiachia. Hakika zilikua ni picha ambazo nilikumbuka matukio yake vizuri sana kwani sio za siku nyingi sana. David akanisogelea na kuanza kuzichambua zile picha na kunionyesha ambapo ilikua ni aibu tupu kwani nyengine tulikua tukipigana mabusu hadharani na kukumbatiana. Kila kitu kilikua kipo wazi, yani sikua hata na neno moja ambalo ningeweza kujitetea.

Umeamua kuujua na undani wangu kabisa Alex, umeamua kuniweka uchi kabisa Alex. Mke wangu wa ndoa!! Unathubutu kutembea na mke wangu kipenzi Janeth!!? Alex!!!

Kiukweli bila kutarajia nilijikuta machozi yakianza kunitoka na kulia kwa uchungu sana kwani yale maneno ya David yalikua yanagusa mpaka ndani kabisa ya moyo wangu. Nilipomtazama David akiwa analia kwa uchungu na kusaga meno ndipo na mimi nilipozidi kutokwa na machozi na nahisi kama ingekua ile gundi ya karatasi niliyofungwa mdomoni, basi ningelia kwa kelele sana.

Mke wangu ana ladha gani Alex!!? naomba uniambie mke wangu ana ladha gani!!?

David aliongea kwa ukali sana kiasi kwamba nikahisi anaweza hata akaniua. Akanitoa kwa nguvu ile gundi mdomoni bila kujali kama itaniletea maumivu na kweli nilihisi kuwa mchubuko juu kidogo ya mdomo na kuanza kuhisi maumivu ambayo kwa wakati huo hayakua na nafasi hata kidogo.

Nikufanye nini Alex, niambie wewe mwenyewe nikufanye nini!!?


David alizidi kuongea kwa ukali na kwa sauti kubwa sana na kunifanya nizidi kuogopa.

Ona sasa familia yangu imegawanyika. Nimemfukuza mke wangu wangu Janeth kwa sababu yako. Juzi kidogo nimpoteze mtoto wangu Winfrida kwa kutoa mimba ambayo wewe ndiye uliyempa. Sasa hivi ni aibu tupu nyumbani kwangu kwani watoto wangu pia wameshajua kama umewachanganya na mama yao. Nyumba yangu haina tena amani niliyoizoea kwa sababu yako wewe mtu mmoja tu. Hivi wewe ni nani Alex!!? Umetumwa na nani Alex!!?

Nisamehe kaka David, naomba unisamehe sana!!

Niliongea kwa kigugumizi sana huku bado nikiwa naendelea kulia.

Shut up!! (Kimyaa!!) Unajua msamaha wewe? Unajua maana ya msamaha!!? Siwezi nikakusamehe kinafiki Alex! Nikikuacha uondoke bila kukufanya kitu chochote utakua msamaha wa kinafiki sana. Najihisi nina deni kubwa sana na ninapaswa kulilipa.

Tafadhali kaka naomba usinifanye kitu chochote kibaya, nionee huruma tafadhali.

Ungekua unajua nini maana ya huruma basi ungeanza kunionea huruma mimi kwanza kabla ya kufikiria kutembea na mke wangu.

Lakini sio mimi niliyetaka, ni yeye mwenyewe ndo amenilazimisha.

Sina haja ya kusikia yote hayo Alex maana kwa sasa hayana maana tena. Najua atakua amekwambia mambo mengi sana kuhusu mimi kwamba sina nguvu za kiume, chumbani simridhishi na kumfikisha anapopataka. Najua atakua amekwambia mambo mengi sana kuhusu mimi na yote hayo ni ya kweli kabisa. Sina nguvu za kiume na simridhishi mke wangu. Kukutana kwetu kimwili ni mwezi hadi mwezi tena itokee bahati sana ndo nasimamisha tena sio kwa uimara unaotakiwa. Nilihisi kuwa huenda mke wangu atakua anaenda kumaliza haja zake sehemu nyengine ila sikuwahi kufikiria hata kidogo kama huyo mtu atakua ni wewe. Siwezi nikakuacha uondoke hivi hivi kwani nitabaki na deni kubwa sana hadi siku nitakayokufa. Naona ni bora tulipane hapa hapa na baada ya hapo nitakua sina tena kinyongo na wewe na nitaendelea na maisha yangu.

Kaka David, tafadhali nipo chini ya miguu yako naomba usinifanye kitu chochote kibaya. Tafadhali nakuomba uwe na roho ya kibinadamu japo kidogo tu kaka.

Kaka!!? Hivi mimi ni kaka yako kweli!!? Hivi mtu unayemuita kaka yako unaweza kumfanyia kitu kama hiki?


Mara nikaona anamuita jamaa mmoja kwa sauti kati ya wale wanne.

Naam boss.

Lete kile kitu.

Nilibaki nalia sana kwani sikujua ni kitu gani alitaka kunifanya, aidha ni kuniua au kunikata viungo vyangu.

Kaka David naomba usinifanyie ubaya wowote tafadhali, nipo chini ya miguu yako na naomba unipe adhabu nyengine yoyote nitaipokea.

Hakuna adhabu nyengine unayostahili Alex zaidi ya hii. Hii ndo adhabu inayokufaa mtu kama wewe.

Mara nikaona yule jamaa akirudi akiwa ameshika box dogo.

Waite na wenzako.

Kweli akaenda kuwaita wenzake na baada ya kama dakika moja nikaona zile njemba nne zote zikiwa zipo mbele yangu.

Mvueni hiyo suruali.

David alitoa amri na kweli wale jamaa wakaanza kunivua. Nikaona sasa kile nilichokifikiria cha kulawitiwa ndo kinaenda kutokea maana niliona zile njemba zipo tayari kwa kazi.

Kaka David usinifanyie hivi tafadhali mimi ni mwanaume mwenzio. Nakuomba nipe adhabu nyengine lakini sio hii.

David hakujibu kitu na nikaona analifungua lile box aliloagiza na kutoa sindano pamoja na vichupa vidogo viwili. Walinivua suruali yote pamoja na boksa na kubaki najiuliza anataka kunifanya nini na ile sindano. Nikaona anainyonya dawa iliyokuwa kwenye vichupa vyote viwili ambazo zilionekana kuwa ni dawa mbili tofauti.

Pindi nitakapokuchoma hii sindano na dawa ikaanza kufanya kazi, utakua upo zaidi ya hivi nilivyo mimi. Hautoweza tena kusimamisha uume wako yani utakua khanithi mpaka utakapoingia kaburini.

Hapana, hapana usinifanyie hivi David adhabu kubwa sana hii kwangu. Uwanaume wangu utakua upo wapi sasa?

Ndo nataka uwe hivyo ili usiendelee kuwaumiza watu wengi zaidi kama ambavyo umeniumiza mimi.


Nililia kwa uchungu sana lakini hakuna aliyejali hata mmoja.

Mtanueni miguu yake.

David alizidi kuwaamrisha wale jamaa na kweli wakatii na wakanitanua miguu na kuziacha wazi kabisa sehemu zangu za siri huku wakiwa wamenibana vilivyo. Ghafla nikasikia simu yangu ikianza kuita kutoka kwenye suruali na David akaamrisha izimwe ili isiwabugudhi wakati wanafanya kazi yao. Kweli jamaa mmoja aliitoa simu na kuikata kisha akaizima. Sikujua hata ni nani aliyekua ananipigia na nilibaki nikiwa nalia sana.

David aliisogeza sindano kwenye sehemu zangu za siri na bila huruma akaiingiza sindano kwenye mshipa mkubwa wa uume wangu ambapo nilipiga kelele sana kwa maumivu niliyoyapata. Aliiminya dawa na ikaingia nyingi sana ambapo nilikua nalia mithili ya mtoto mdogo. Akaichomoa sindano na kuongeza ile sumu ambayo mwanzo nilifikiri ni dawa na kuinyonya tena kwenye sindano. Akanisogelea tena na kuiingiza sindano kwenye korodani zangu zote mbili na kuiminya sumu yote. Kiukweli yalikua ni zaidi ya machungu kupoteza urijali wangu na waliponiacha nilidondoka chini kama mzigo nikiwa nipo na kiti nilichofungwa na kuendelea kulia kwa sauti sana. Hakika yale yalikua zaidi ya machungu kwenye maisha yangu na lilikua ni kovu ambalo kamwe haliwezi kufutika.

Na kuhusu milioni 25 zangu ulizoniibia sina kitu cha kukufanya zaidi ya kwenda kukukabidhi polisi maana wanakutafuta sana kwa mauaji uliyoyafanya. Alex wewe ni zaidi ya mnyama mkali ambaye hana huruma hata kidogo. Naamini kidonda changu kinaweza kikafutika ila kidonda chako kitadumu milele na milele. Na nakuahidi kuwa familia yangu itasimama tena imara zaidi ya mara kwanza na mke wangu nitamrudia tena. Asante sana kwa kila kitu Alex, nimekutana na wewe, umenifundisha na nasonga mbele. Sina majuto ila ni somo jengine kwenye maisha yangu.

Jamani naomba huyu akae hapa kwa siku tatu na Ijumaa nitakuja tena hapa kumchukua ili nikamkabidhi kwa polisi wafanye kazi yao. Acha hii sumu ifanye kazi vizuri na kupotea mwilini ili tupoteze ushahidi wa hiki tulichokifanya.

David aliwaambia wale jamaa na kuagana nao kisha akatoka mule chumbani. Nilibaki nikilia kwa uchungu sana huku nikijuta sana kwa yote yale niliyoyafanya. Wale jamaa waliniinua na kunivalisha nguo kisha wakanikalisha tena kwenye kiti na kunifunga kamba vizuri kama mwanzo na wakatoka nje na kuniacha peke yangu nikiendelea kulia.


************* **************


Kweli baada ya siku tatu David kama alivyoahidi, alikuja na kwa kushirikiana na wale jamaa walinipeleka mpaka kituo cha kati (maarufu kama Central) na kunikabidhi kwa polisi huku akifungua jalada la kumuibia pesa taslimu, milioni 25. Kiukweli zilikua ni milioni 33 nilizoziiba ila nahisi alijichanganya kidogo kwenye mahesabu yake ila kwa wakati huo zilikua hazina maana tena kwangu.

Polisi waliwashukuru sana wakina David kwa kuweza kunikamata kwani nilikua ninatafutwa sana nchi nzima. Baada ya kuandikisha kila kitu, waliondoka na mimi nikaenda kuswekwa rumande ambapo nilikuta kumejaa watu wengi sana. Asikwambie mtu yale maisha sio mazuri kabisa kwa binadamu kwani watu wengi niliowakuta mule walikua wamedhoofu sana.


Baada ya kama wiki moja ikatoka oda kuwa ninahitajika mahakama ya mkoa wa Tanga kwa ajili ya kusikiliza kesi yangu ya mauaji na ilibidi nipelekwe huko. Nilisindikizwa kwa ulinzi mkali sana kiasi kwamba sikuamini kama mimi ndiye niliyekuwa nafanyiwa mambo yote yale. Tulifika salama Tanga na baada ya siku kadhaa nilifikishwa mahakamani na kuanza kusikiliza kesi yangu. Nilihudhuria mahakamani kama mara nne mfululizo bila hukumu kutoka na siku zote nilikua nikirudishwa mahabusu tu. Nilimuona askari mmoja gerezani hapo akiwa na roho nzuri sana na ilibidi nimuite ili niongee nae.

Afande samahani sana nina shida kubwa sana naomba unisaidie.

Shida gani hiyo?

Naomba niwasiliane na mke wangu maana hajui kitu chochote kilichonipata. Ni muhimu sana afande maana nina maagizo ya muhimu sana.

Hapana kwa kesi yako siwezi nikakupa simu uongee nitaingia matatizoni sana. Nipe namba yake ya simu nitampigia mimi.

Kweli nilimtajia namba ya simu ya Vanessa na kumpa maelekezo yote na tukaweza kuelewana.


Ilipofika siku ya Jumapili ambayo ndo huwa siku ya kutembelea watu gerezani, nilipata ujumbe kuwa kuna mgeni wangu. Nilitoka kwa shauku sana na kwenda kumuona ambapo nilikutana uso kwa uso na Vanessa. Vee aliponiona alishindwa kabisa kujizuia kwani alianza kulia sana hadi na mimi nikajikuta machozi yakiwa yananilenga.

Nyamaza mke wangu, be strong. (Kuwa imara.)

Kwakua muda wa kuonana ulikua mfupi sana ilibidi Vee anyamaze na kuanza kuongea nae.

Vipi Kelvin umemuacha wapi?

Nimekuja nae ila wamenizuia kuingia nae nimemuachia dada wa mapokezi.

Niliinama chini kwa huzuni.

Vipi nyumba ulifanikiwa kuiuza?

Hapana bado.

Basi usiuze tena sitisha huo mpango. Sidhani kama nitarudi tena huko.

Vee alikua analia sana kiasi hadi nikawa namuonea huruma kuliko hata ninavyojionea huruma mimi mwenyewe.

Akaunti yangu benki ina kama milioni 20 na zaidi na pia ndani kuna zile milioni 10. Namba ya siri ya ATM ni 7788. Naamini hizo zitakusaidia kuanza maisha wewe pamoja na mtoto. Pia mama utamkumbuka kumpelekea angalau milioni 5 maana mara ya mwisho nilivyoenda nilimuachia milioni 5. Mwambie mama nampenda sana na asijali mtoto wake nitakua salama.

Maneno yangu yalizidi kumtoa machozi Vanessa.

Samahani sana Vanessa kwa kutoijua thamani yako mapema. Hakika sikutegemea kabisa kama wewe ndiye ungekua na mimi kipindi kama hiki. Nakupenda sana Vanessa na nitakupenda kwa siku zote za maisha yangu.

Nakupenda pia Alex.

Vee alijibu kwa uchungu sana kiasi kwamba nilihisi machozi yakianza kunitoka.

Hey hey hey!! Haya muda umeisha tokeni haraka.

Aliongea afande mmoja kwa amri.

Vee alianza kurudi nyuma taratibu huku akiwa analia sana.

Naomba umuangalie mwanangu Vee, unapopata nafasi naomba umpeleke kwa bibi yake. Take care of yourself. (Kuwa makini na wewe mwenyewe.)

Vee hakujibu kitu na aliondoka huku akiwa analia sana na kuniacha na huzuni kubwa.


*************** ***************


Siku ya hukumu ilifika mahakamani ambapo kama kawaida watu walikua ni wengi sana. Nilikutwa na kesi mbili, ya kwanza ni ya mauaji kwa kutumia silaha na ya pili ni kesi ya wizi.

Kilichonishangaza siku hiyo ni kuwakuta watu nisiowatarajia kuwepo kabisa pale mahakamani ambapo David alikuja na familia yake yote kasoro mtoto wao mdogo tu Patrick. Walikaa pamoja na mke wake Janeth, Happy pamoja na Winfrida. Kilichonishangaza zaidi ni kumuona Agness nae yupo pale mahakamani tena akiwa amekuja na mama yake. Kiukweli ilikua ni zaidi ya kuchanganyikiwa, aibu na fedheha. Hakimu alianza kusoma kesi na alihitajika mke wa marehemu Shaffih ili akatoe ushahidi na Agness alisogea kizimbani.

Bibi Agness, unamfahamu vipi mtuhumiwa?

Aggy alikohoa kidogo kisha akaanza kuongea.

Mheshimiwa hakimu, mtuhumiwa aliwahi kuwa mpenzi wangu na tuliishi wote kijiji kimoja.

Sawa. Maelezo yako uliyoyatoa polisi yanasema mtuhumiwa aliwahi kuja nyumbani kwako na kufanya ugomvi mkubwa sana kwa marehemu mume wako.

Ndio mheshimiwa.

Siku ya mwisho ya uhai wa marehemu mume wako nini kilitokea?

Marehemu alinitaarifu kuwa kuna mtu asiyemfahamu amempigia simu na anataka kumpa tenda ya kutengeneza madawati ya shule yake.

Marehemu alikua ni fundi seremala?

Ndio mheshimiwa.

Endelea.

Wakakubaliana wakutane usiku maeneo ya Donge ambapo kweli ilipofika mida ya saa 2 usiku ndo aliondoka nyumbani. Nilimsubiri sana kwa usiku kucha mpaka kulipopambazuka ndo nikapata taarifa kuwa mume wangu ameuawa.

Aggy alikua anaongea lakini anaonekana hayupo sawa hata kidogo. Hakimu alimuhoji maswali mengi hadi alipojiridhisha akamruhusu aende kukaa.

Ushahidi wote umekamilika, tuna ushahidi wa simu ya mwisho kabisa ambayo marehemu alipigiwa, namba yake ilisajiliwa kwa majina ya Alex Msare. Pia tuna ushahidi wa video kwani eneo tukio lilipotokea kwa bahati nzuri kuna nyumba imefungwa camera za CCTV na imenasa tukio lote mpaka sura ya mtuhumiwa. Mahakama yangu imekukuta na makosa mawili ndugu Alex Msare. Kosa la kwanza ni kuua kwa kutumia silaha na kosa la pili ni kuiba pesa taslimu shilingi milioni 25 mali ya ndugu David Aloyce.


Hakimu alinisomea mashitaka yangu na kunitajia aina ya vifungu vya sheria vinavyoendana na kosa langu.

Kwa kufuata vifungu hivyo vya sheria, ninakuhukumu kifungo cha maisha jela bila msamaha na adhabu ya viboko 30 wakati unaingia.

Bila kutegemea nilijikuta nikidondoka pale kizimbani niliposimama na kukaa chini ambapo machozi yalianza kunitoka mfululizo. Nilipotazama upande wa kina David, niliona David na mke wake wakiwa wameinama chini kwa huzuni huku Happy na Winfrida wakishindwa kujizuia na kuanza kulia. Nilipomtazama Agness ndo alikua hajiwezi kabisa ambapo kilio chake kilianza kuwa kikubwa mpaka akainuka na kuanza kukimbia kutoka nje. Muda huo huo hakimu aligonga nyundo kuashiria kuwa hukumu imepita na askari magereza wakanifuata na kunifunga pingu kisha wakaanza kunitoa nje na kupitishwa mahali walipokaa David na familia yake.

I'm sorry, i'm so sorry! (Samahani, samahani sana!)

Niliwaambia wote kwa ujumla huku nikiwa nalia sana. Nilitolewa nje ya mahakama na kupakizwa kwenye karandinga la magereza na kuletwa hapa gerezani Maweni. Tangu kipindi hiko mpaka sasa uume wangu haujasimama tena yani nimekua khanithi.


Daah!! Aisee pole sana Alex. Story yako inasikitisha sana ndugu yangu yani mapenzi tu ndo yamesababisha mpaka leo upo hapa!!

Asante sana Isack. Mapenzi tu ndo yamenifanya leo naishi huku kwenye giza. Ila namshukuru Mungu mwaka mmoja na nusu sasa tayari nimeshazoea maisha ya huku.

Vipi kuhusu rafiki yako James?

James nilimuacha Dar es salaam anafanya shughuli zake. Natamani hata kujua mama yangu anaendeleaje. Natamani kujua mtoto wangu Kelvin na Vanessa wanaendeleaje lakini huku tulipo haturuhusiwi kutembelewa kabisa.


Wakati bado tunaendelea kuongea, tulisikia kengele ya kuingia ndani ikigongwa. Mida hiyo ya saa 9 alasiri ndo huwa muda wa kwenda kulala kila siku na kuamka saa 11 alfahiri. Tuliinuka na kuanza kuelekea kwenye sero yetu mimi na Isack. Kila kitu kwenye maisha yangu kimebaki story tu na kila aina ya majuto.


********** MWISHO *********


1 comment:

  1. Story hii imenipa mafunzo mengi sana ikiwemo mapenzi,usaliti,visasi na kingine ni lazima tutambue thamani na umuhimu wa kila mtu ulienae ktk maisha yako..

    ReplyDelete

BLOG