Search This Blog

Saturday, February 26, 2022

GENGE - 2

   *

Simulizi : Genge 

Sehemu Ya Pili (2)


Timu nzima ya TSA ilifanya kjazi ngumu sana mpaka kuweza kutambua Vincent Mwanachia anaishi kwa kificho huko Lisbon, Ureno. Baada ya Madam S kupeleka tafutishi hiyo kwa Mkuu wa nchi, ikaandikwa hati ya kifo chake kufuatia hukumu ya mwaka 1984.

Ndani ya jiji la Lisbon, mwaka 2003, Kamanda Amata anakuwa kwenye kibarua kilekile kama cha Brussels. Mara alipotoka bafuni kuoga na kujiweka sawa katika mavazi ya kawaida, alitupia tena jicho kwenye vile vikolokolo alivyovipata kwa wale marehemu. Mara hii akaona kitu kisicho cha kawaida katia ya vile pale mezani. Casino Lisboa. Kipande cha karatasi kiliandikwa hivyo. Akakitazama mara kadhaa, akakihukua na kukikunjua vizuri, akakisoma upya.

Kwa nini mwanzo sikuona umuhimu wake? Akajiuliza. Kuna lolote ninalotakiwa kufanya kule? Akajikuta njiapanda. Akiwa katika hali hiyo, akashtushwa na hodi iliyobishwa mlangoni. Amata akakusanya vile vitu na kuvifungia kwenye droo. Akajiweka tayari na kuuendea mlango uliokuwa ukigongwa kwa fujo. Taratibu, Amata akaufungua na kumruhusu agongaye aingie. Dana. Dana aliingia ndani ya chumba hicho akitweta. Akageuka na kumtazama Amata aliyekuwaakikunja mikono ya fulana yake ya pull neck.

“Umefanya nini Amata?” Dana akauliza kwa tashwishwi. Amata akafanya kama hajasikia swali hilo. Alipomaliza kukunja mikono ya fulana, akachukua saa yake na kuivaa. Dana akasimama mbele yake, uso kwa uso.

“Nakuuliza Amata, husikii?” akauliza kwa sauti ya ukali. Amata akamaliza kuvaa saa yake na kuchukua koti la jinzi, akalivaa na kuliweka sawa. Dana akajitupa kitini na kubaki akimtazama kijana huyo. Alipomaliza kujiandaa, akavuta mkoba wake na kutoa bastola yake aina Beretta Pico na kuipachika kwenye mkwiji wa suruali yake. Akamgeukia Dana na kumtazama.

“Mbona unaingia ndani kwa mtu unapia makelele, we una kichaa?” akamtupia swali. Dana akabaki kimya akitazama tambo la kijana huyo shababi, aliyesimama imara pasi na kutetereka.

“Umeua askari mbele ya CCTV camera, umeharibu kila kitu, wanakutafuta kila kona,” Dana akalalama akiwa kaegemea kiti kile na kupumua kwa nguvu.

“Sijaua askari, wamenifananisha!” Amata akajibu.

“Umeua Amata,” akamwambia na kumwekea picha mezani. Amata akazitazama zile picha kutoka mbali. Akajiona katika picha tatu tofauti katika tukio lile.

“Dana!” akaita.

“Unasemaje?” akamuuliza.

“Unapoongea na mwanaume, uwe mtulivu. Sasa sikiliza, kuanzia sasa ninatengua mission ambayo ninyi mliipanga,” aliposema hayo, Dana akabaki katoa macho.

“Hah, unasemaje? Unapaswa kufanya lile tulilolipanga,” Dana akasimama na kuonea kwa mamlaka.

“Sikiliza, narudia, kuanzia sasa ninatengua mission ambayo ninyi mmeipanga...”

“Halafu ufanyeje?” Dana akamkatisha kwa swali.

“Narudi Tanzania, usiku huu...”

“Una kichaa!” Dana akang’aka.

“Kichaa unacho wewe na bosi wako ambao mmevujisha siri hii kwa Mwanachia...” Amata akamwambia.



Narudi Tanzania, usiku huu...”

“Una kichaa!” Dana akang’aka.

“Kichaa unacho wewe na bosi wako ambao mmevujisha siri hii kwa Mwanachia...” Amata akamwambia.

“Unasemaje!” Dana mishipa ikamtoka, “Sisi tunaweza kufanya upuuzi kama huo?” akauliza.

“Sikiliza Dana... hii kazi mimi nimeifanya miaka mingi kuliko wewe, usifikiri kuwekwa mkuu wa usalama katika ubalozi wetu hapa Ureno ndo umefika. Mimi siyo renki yako, sawa?Hebu nambie, hizi picha wewe umezipata wapi? Ina maana ulikuwa unajua mchezo mzima unaotakiwa kutukia kwangu. Pili, safari yangu ya kuja huku hakuna aliyekuwa anaijua zaidi ya ofisi yako tu, Mwanachia na genge lake wamejuaje kama nipo hapa? Mbona Brussels nilifanya kazi peke yangu na sikujulikana?

Mpo matatani! Yaani mpo matatani...” Amata akaonea kwa ukali na kumfanya Dana kunywea kabisa. Maneno yaligonga mfupa.

“Nani aliyekwambia huo uongo wote?” Dana akajikakamua kusema.

“Uongo? Balozi Asantino Mwampamba, yaani bosi wako, alikuwa kikosi kimoja na Vincent Mwanachia. Yeye alimtangulia tu kuingia jeshini, ni marafiki, wanafahamiana, siwezi kushangaa wakilindana. Nimetenua mission narudi Tanzania,” akamwambia Dana huku akitoa tiketi ya ndege na kumtupia mezani. Dana alipoisoma, ni kweli, ilikuwa ya usiku huo huo.

“Nipeleke Uwanja wa ndege...” Amata akamwambia Dana ambaye sasa hakuwa yale maneno. Amata akainua mkoba wake na kumpa ishara ya kutoka.

“Yaani hata sikuelewi we mwanaume!” Dana akasema huku akiinuka.

“Nipeleke, kama hutaki nitakodi taksi. Na ndipo nitapopata uhakika wa maneno yangu,” Amata akamwambia huku tayari wakianza kutoka hotelini hapo. Baada ya kuweka mambo yote ya hotelini hapo, Dana na Amata wakaelekea Uwanja wa ndege.

“Asante sana Dana! Fikisha salamu zangu kwa Mwampamba...” Amata akamwambia Dana wakati wakiagana katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Lisbon.

“Sawa!” Dana akajibu, kisha akamsindikiza mpaka ndani ya uwanja huo na kuhakikisha amemaliza hatua zote za safari.

“Waweza kwenda Dana, nisikucheleweshe na shughuli zako,” Amata akamwambia yule mwanamke.

“Usiwe na wasiwasi, kwa kuwa ilikuwa kazi yangu kukuhost sina budi kukuescort pia...” akamjibu.

Nusu saa baadae, sauti ya mwaDanada ikasikika kwenye vifaa maalumu ikiwataka abiria wote wanaoondoka kuelekea Addis Ababa waingie ndegeni. Kamanda Amata, akamkumbatia Dana na kumbusu shingoni kisha akamwacha na kuelekea katika lango ambalo lingemfikisha pale ndege ilipo. Mita chache kabla ya kuufikia mlango wa ndee hiyo, Amata akafungua mlango mdogo na kutoka nje. Akateremka ngazi mpaka eneo ambalo gari za kukokota mizigo zimeegeshwa. Akiwa anaambaaambaa na ukuta huo, akakunja kona na kuingia katika mlango wazi. Moja kwa moja akaibukia katika chumba ambacho inafikia mizigo. Wafanyakazi wa eneo lile wakataka kumzuia, akajitambulisha na kuwaonesha kitambulisho cha kidiplomasia. Wakamwongoza na kumwonesha njia ya kutokea nje kupitia upande huo.

Upande wa nje kulikuwa na watu wengi na wanafika kupokea na kusindikiza wageni. Giza lilikuwa limemezwa na taaza zenye mng’aro wa dhahabu. Amata akapepesa macho kama atamwona Dana. Akasimama palepale alipo akiangaza kwa umakini , kikachero. Haikuchukua muda, macho yake yakamnasa mwanamke huyo.

Dana alikuwa akitembea haraka haraka huku nyuma akifuatiwa na kijana mmoja. Kutokana na wingi wa watu, Dana alipotea katika macho ya Amata. Amata naye akajitoa pale aliposimama na kuvuta hatua mpaka upande wa pili wa maegesho. Akatembea haraka haraka huku akipita viunga vya maua. Katikati ya magari mengi, kulikuwa na Volks Wagen moja likiwasha hazard. Alipolikazia macho zile taa zikazimika kisha zikawaka zile kubwa kwa mtindo wa flash, akaelewa. Akaliendea na kuingia katika kiti cha mbele, pembeni ya dereva. Ndani ya gari hili kulikuwa na mtu mmoja tu, mwanamama.

“Welcome on board sir... I will fly you safely to Addis’”Madam S akamwambia Amata na wote wakaangua kicheko.

“Ni kuwacheza shere tu, na nataka usiku huu huu nifunge kazi,” Amata akamwambia Madam S.

“Utaanzia wapi?” akauliza.

“Casino di Lisboa!” Amata akajibu.

“Kuna chambo?”

“Bila shaka... nahisi mwanzo utakuwa mzuri. Sasa tupo TSA peke yetu kwenye mchezo huu...” Amata akamwambia Madam S.

“Wataiona ngondo...” Madam S akamalizia huku akiliondoa gari lile maegeshoni na kurudi mjini Lisbon.

* * *

. Mtu mzima , Vincent Mwanachia, mpiganaji wa Jeshi la Tanzania aliyeasi, aliwasili katika Casino kubwa na la kisasa jijini Lisbon. Pembeni yake akiwa na Bi. Jesca Tibatulanwa, mwanaharakati mwenye ulimi wa moto. Anayeweza kushawishi na kukubalikana watu wa rika lote.

“Mbona Casino?” Jesca akauliza.

“Kuna wadau wa kuweka nao mambo sawa hapa, kisha mimi na wewe kesho tutasafiri kukutana na wanachama wengine. Kama ulivyoambiwa na mkuu kuwa tuna mkakati wa aina nyingine katika kutimiza azma yetu,” Mwanachia akamwambia Jesca. Muda huo huo, kijana mmoja akajitokeza kuwapokea na kuwaongoza kuingia ndani ya jengo hilo.

Jengo lilipambwa kwa mataa ya kila aina. Watu wengi walikuwamo wakicheza kamari za aina aina. Kila aliyekuwa hapo, alionekana ni mwenye nazo. Kulikuwa na starehe. Wadada waliovaa nusu uchi walikuwapo. Na wale wasiovaa kabisa, nao walikuwapo. Vinywaji vya kila aina vilikuwa vikipitishwa huku na kule kwa walioagiza. Waliohitaji huduma ya makahaba nao walikuwa na nafasi yao, ili mradi ushetani wote ulikuwa ndani ya jumba hilo.

Katikati ya ukumbi huo kulikuwa na meza kubwa ya Poker. Mchezo wa vibopa. Mwanajeshi mstahafu, Vincent Mwanachia, aliongozwa mpaka kwenye meza hiyo ambayo kwa muda huo ilikuwa na watu wengine wanne. Walinzi wake, wakazunguka mita moja nyuma ya meza hiyo wakiungana na wengine waliwakuta hapo.

“Karibu sana Comrade!” sauti nzito, iliyojawa mikwaruzo ikamtoka mmoja wa wazee aliyeketi mkabala na Mwanachia. Mzee yule mwenye kichwa kisicho na nywele,alikuwa mara kwa mara akipachika kinywani kifaa cha kuvutia dawa ya pumu.

“Nimekaribia,” Mwanachia akajibu.

“Pole sana kwa ajili ya vijana wako,” akamwambia huku akitoa ishara aletewe kinywaji maana alikuwa amesawajika uso wote.

“Mwanaharamu yule, ana bahati sana amekimbia,” Mwanachia akasema.

“Una uhakika?” yule bwana akaonesha hali ya mshtuko kidogo.

“Yap! Mtu wangu mmoja amenihakikishia hilo kwa kuwa amempeleka mpaka uwanja wa ndege. Na ameondoka na Ethiopia Airline,” Mwanachia akmweleza yule mzee.

Nje ya ukumbi ule, Kamanda Amata bado alikuwa ndani ya gari pamoja na Madam S.

“Ok, ngoja niingie ndani, nitakujuza nitakachokiona,” Amata akamwambia Madam S.

Alipotaka kufungua mlango ili atoke nje ya gari lile, akasita kidogo na kurudi ndani. Wakati akifanya hilo likapita gari moja kwa kasi mbele yao.

“Dana!” akatamka.

“Dana?” Madam akauliza kwa kutaka uhakika.

“Yes! Dana. Sasa naanza na yeye, lazima nijue anafuata nini huku,” Amata akasema. Alipotaka kutoka, Madam S akamgusa bega, akampa mzula na miwani.

“Chukua hivi, vaa mara moja. Una bastola?”

“Ndiyo ninayo,”

“Ongeza na hii...” Madam S akampa bastola nyingine, Marksman. Bastola toleo jipya wakati huo, yenye uwezo wa kusafirisha risasi kwa futi 250 kwa sekunde.

Amata akateremka, akavaa ule mzula na kuipachika miwani usoni pake. Alipopachika mikono mkifukoni, akavuka barabara na kuelekea upande wa jumba lile huku akiangaza macho kuona ni wapi Dana ameegesha gari lake. Hakuchukua muda, akaliona. Akajibanza kwenye maari mengine ili aone nini kinaendelea. Alichokishuudia, ni Dana akibishana na vijana wawili wa Kizungu. Akasubiri. Dakika mbili baadae, wakaongozana pamoja kuingia ndani ya jengo lile, naye akawafuata kwa kupita upande wa pili. Walipofika mlango mkuu, wakaingia ndani, nao ukajifunga.amata akawahi , akaingia pia. Baada ya mlango wa kwanza , kulikuwa na mwingine. Kilichomshangaza ni kuwa milango yote haikuwa na ulinzi.

Haiwezekani! Akawaza. Amata akajua wazi kuwa kama hakuna walinzi katika milango hiyo, basi kwa vyovyote anepambana nao mahali pengine. Akaingia na kujikuta kwenye ukumbi ule ule ambao Mwanachia alikuwamo. Hatua zake zikamfikisha katika kaunta kubwa ya vinywaji.

“Um copo de vinho tinto,” akaagiza mvinyo nyekundu. Akaletewa chupa ndogo na bilauri.

Pamoja na kunywa huko, macho yake yalikuwa yakiangaza huku na huko. Mara kwa mara yalikatishwa na wasichana warembo waliokuwa wakikatiza mbele yake. Akaanza upya kutazama, huku akihakikisha hagunduliki na mtu. Wakati akiendelea kutazamatazama, akajikuta akiguswa na bomba dogo la baridi ubavuni mwake.

“Termine sua bebida e vá...” akaambiwa amalize kinywaji chake waondoke. Kamanda Amata akajua tayari keshaingia mikononi mwa majahili. Hakutaka iwe hivyo lakini imebidi. Akawa mpole.

“Não se preocupe, apenas fique em paz,” akawajibu, wasiwe na wasiwasi bali wawe na amani tu.

Dakika kumi baadae, akamaliza kinywaji chake, wakamtaka ateremke kwenye kiti alichokikaa. Akafanya hivyo. Wale jamaa wakamwongoza taratibu upande mwingine wa ukumbi ule. Wakaingia naye kwenye lifti. Humo wakawakuta vijana wengine wawili. Kimya, hakuna aliyekuwa akiongea. Lifti ile ikapanda mpaka ghorofa ya tatu, wakatoka na kumwongoza mateka wao mpaka katika chumba kimoja wapo.

Ndani ya chumba hicho walimkuta Vincent Mwanachia, Dana , yule mzee wa kwenye kamari pamoja na vijana wengine wawili. Ukijumlisha na hawa wanne wanakuwa watu tisa. Vincent Mwanachia, akaanza kupiga makofi na wale wengine akiwemo Dana wakafanya vivyo hivyo. Cumba hiki kikubwa kiasi hakikuwa na samani yoyote zaidi ya viti viwili vilivyokuwa vimekaliwa na Mwanachia na yule mzee.

“Karibu sana kijana!” Mwanachia akamwambia Amata. Amata hakujibu, akabaki kumtazama tu.

“Hata usipojibu, umeshaingia kwenye mikono ya shetani, hutatoka humu. Tumekuwa tukikusaka sana tangu ulipomuua Titus Mwakibinga. Na sasa umejileta mwenyewe...” Mwanachia akaongea kwa Kiingereza ambacho wote walielewa vyema.

“Mbona unaongea maneno mengi? Mimi nimekuletea barua yako tu kutoka nyumbani...” Amata akamjibu.

“Barua!” Mwanachia akashangaa. Akawatazama wenzake kisha wakaanza kucheka. “Iko wapi hiyo barua?” akamwuliza.

“Mfukoni, mwambia kijana aje achukue akupatie,” Amata akamwambia. Mwanachia akampa ishara Dana akachukue barua hiyo. Dana alipoanza kuvuta hatua kumwendea Amata, wale vijana sita, wote wakachomoa bastola kumwelekezea Amata. Dana akamfikia Amata na kuingiza mkono mfukoni, akachomoa bahasha na kumpatia Mwanachia. Mzee huyo akaichana na kuitoa karatasi ya ndani, akaifungua na kuanza kuisoma. Chumba kizima kilikuwa kimya, ni bastola tu zilikuwa zikimtazama Amata. Mwanachia alipomaliza kuisoma karatasi ile akaitupa chini kwa hasira. Akavuta kamasi ndani.

“Hamuwezi, na bado tutaikomboa nchi yetu... muda si mrefu mtashuhudia mapinduzi makubwa,” Mwanachia akasema.

“Na mapinduzi hayo hutayashuhudia hata kidogo... kwa kuwa una masaa mawili tu ya kuishi. Hizi bastola zote, zitakugeukia wewe muda si mrefu,” Amata akasema.

“Pumbavu sana wewe!” yule mzee mwingine akasema.

“Hata kama! Ila hukumu ya rafiki yako ni kifo, na siku ya kifo chake ni leo...” Amata akamwambia yule mzee.

Yule mzee kwa hasira, akarusha kile kidubwana anachotumia kuvutia dawa ya pumu, Amata akakidaka na kupiga msamba akakaa chini. Risasi za wale jamaa zikapita hewani na kuchimba ukuta.

Kabla hawajajiweka sawa, tayari kamanda alijizungusha kiufundi na kumchota ngwala mmoja. Akaenda chini mzima mzima, Amata akamdaka na kukikunja kiganja chake. Akaikamata bastola ile kwa ufanisi, risasi ya kwanza ikafumua kifua cha jamaa mwingine aliyekuwa mbioni kufyatua yake. Chumba kilijazwa na taharuki, mtafutano.

“Muueniiiiii” Mwanachia alipiga kelele. Yule mzee mwingine akabaki kukohoa tu na kupumua kwa shida. Pumu ilimkamata. Kamanda Amata, akabingirika na yule jamaa huku akifyatua risasi hovyo. Kwa makusudi alikuwa akipiga juu. Mara vifaa vya zimamoto vikaanza kumwaga maji na ving’ora vya hatari vikaanza kupiga kelele. Balaa. Upinzani ukaanza kuongezeka, amata akaona isiwe shida, akachomoa bastola na kuanza kazi.alikuwa na nafasi nzuri ya kumuua Mwanachia lakini aliaswa na mama yake asifanye hivyo alitii. Beretta pico ikatema risasi na kumwangusha kijana mwingine huku wengine wakiwahi mlango akiwamo Dana.

Amata akajiviringa chini mpaka kwa Mwanachia akainuka na kumkamata ukosi wa shati. Akamuinua.

“Walinzi wako wote wamekuacha!” Amata akamwambia. Mwanachia akabaki akitetemeka. Vishindo kutoka kwenye korido vya watu wanaokimbia vikamgutusha Amata. Akamwinua Mwanachia na kwa nguvu zote akajirusha nae dirishani. Kioo kikatawanyika huku risasi mfululizo zikimkosakosa.




Walinzi wako wote wamekuacha!” Amata akamwambia. Mwanachia akabaki akitetemeka. Vishindo kutoka kwenye korido vya watu wanaokimbia vikamgutusha Amata. Akamwinua Mwanachia na kwa nguvu zote akajirusha nae dirishani. Kioo kikatawanyika huku risasi mfululizo zikimkosakosa.

“Amekimbiaaa, muwahini chiniiii,” mmoja wa wale walinzi akapiga kelele. Wote wakageuza na kuanza kueteremka, kurudi walikotoka.

* * *

Ndani ya jengo hilo kizaazaa hakikuwa cha kawaida, watu walikimbilia nje. Pindi tu Madam S aliposhuhudia mtifuano ule kupitia runinga ndogo ndani ya gari iliyokuwa imeunganishwa na ile miwani aliyompa Amata, akawasha gari na kuondoka zake.

Huku nyuma aliacha tafrani nzito, kila mmoja akipigania uhai wake. Ni muda mfupi sana , lile eneo lote likazingirwa na polisi na zimamoto. Usalama ukazingatiwa.

Upande wa pili wa jengo lile, Kamanda Amata alitua chini akiwa kamkumbatia Mwanachia. Maua marefu ya liyotengenezwa vyema yaliwapokea, ikawa salama yao. Kwa kuwa haikuwa mbinu ambayo Amata aliifikiria kuifanya, lakini kutokana na mazingira ikambidi.

Hakupoteza muda, akavirinika chini na kumkuta mtu wake akihema ovyo. Alipogeuza macho huku na kule hakuona jinsi ya kutoroka eneo lile maana gari lilikuwa upande wa pili. Akajilaumu kwa kosa alilofanya. Akiwa katika kuamua nini afanye, akasikia sauti kali ya matairi ya gari takisuguana na barabara.

“Spaaarrrrkkkk!” sauti ikamwita, alipogeuka barabarani hakuamini anachokiona. Scoba. Kasimama pale na BMW Sports. Kamanda Amata akampa ishara ya kufungua buti. Scoba akafanya hivyo. Kwa nguvu zote akamnyanyua Mwanachi na kuvuka naye bustani ile mpaka barabarani, akamtumbukiza kwenye buti na kulifunga. Akawahi mlango wa abiria na kuingia. Scoba akapia norinda, kabla hajaweka gari sawa, akashuhudia kioo cha nyuma kikimwaika, risasi.

“Twende!Twende!” Amata akamwambia huku akifyatua kiti na kukilaza. Scoba akapita katikati ya maua na kutokea upande wa pili. Kwa kutendo hicho akawapoteza shabaha wajinga wale. Alipokuja kukaa sawa barabarani, akataka kupenya katika ya majengo mawili ili atokee barabara kuu. Akajikuta akikutana na gri jingine uso kwa uso, hakuna pa kupita. Akapiga rivasi lakini badala yake akagonga gari la nyuma. Hakusimama, akakanyaga mafuta kurudi nyuma huku lile gari la mbele yao likizidi kuwakaribia na wale jamaa wakajitokeza nusu madirishani wakiwa na bunduki aina ya Aptus mikononi.

“Kamanda, Ambush!” Scoba akasema.

“Usijali, we fanya hivi hivi mi nitawafanyia kazi!” akamjibu, “Una bunduki?” akamwongezea swali.

“Kuna Wilson Combat, ipo full !” akamjibu.

“Eeeewaaah!” Amata akashukuru na kuichomoa kutoka ilipohifadhiwa. Akashusha kioo aikwa bado amelala na kiti. Scoba alikuwa akichezesha tairi kwa mtindo ambao wale jamaa walijikuta wanashindwa kupata shabaha.

“Shoo inaanza! Moja , mbili, tat...” kabla hajamaliza alishuhudia kioo cha mbele cha gari lao kikitawanyika. Sekunde hiyo hiyo akaitumia, akainuka ghafla na kuchia riosasi moja tu. Aikukosea, ikpenya katikati ya paji la uso wa dereva. Lile gari likayumba mara ya kwanza na lilipoyumba mara ya pili, likajipiga katika ukingo wa barabara na kuinuka upande mmoja. Amata akaweka shabaha nyinine na risasi ya pili ikafumua tanki ya mafuta. Moto mkubwa ukalipuka. Lile gari likpaishwa juu na kuteremka chini kama mzigo.

Scoba akazungusha gari na kuingia barabara ya Oceanos. Kasi aliyokuwa akitembea nayo ilikuwa ya kuogopesha. Hawakufika hata mwendo wa dakika kumi, tayari maari ya polisi yalikuwa nyuma yao. Kutoka katika magari yale, walisikia matangazo ya kuwataka kuweka gari pembeni.

“Oh Shiiit!” Scoba akatamka aliposikia amri hiyo.

“Usisimame, fanya unachoweza, uwapoteze,” Amata akamwambia. Scoba, akaongeza kasi, akaanza kufanya overtaking za hatari. Alipolipita gari la tatu, lile gari likafunga breki na kusimama ghafla. Kishindo kikubwa kikasikika, kikafuatiwa na kingine. Ilikuwa ajali, iliyohusisha magari manne yakiwemo ya polisi.

“Safi sana! Nakuaminia siku zote pilot wangu,” Amata akampongeza Scoba. Akageuka nyuma kutazama kama kuna anayewafuatam, hakuna. Scoba akaiacha barabara kuu na kuingia barabara ndogo.

“Vipi?” Amata akauliza.

“Katika barabara kuu kama ile, kamera za usalama ni nyingi, hatutaweza kufanikisha misheni yetu,” Scoba akajibu huku akipita barabara yenye vumbi jingi, kandokando ya machimbo ya mawe.

“Angalia katapila tu!” Amata akaongea kwa woga baada ya kuona mwendo wa Scoba na jinsi anavyoyapita maskaveta.

“Upo salama braza, shaka ondoa!’ Scoba akajibu huku akikunja kona kali na kuingia kwenye handaki refu na kubwa, lenye uwezo wa kupitisha magari sita kwa wakati mmoja. Nyuma yao wakasikia kishindo kikubwa na vumbi likitimka. Ajali mbaya ilitokea kati ya gari moja dogo lililokuwa likiwafuatilia kugongana uso kwa uso na skaveta la kutengeneza barabara. Ndani ya gari kulitawaliwa na ukimya, Scoba aliendelea kucheza na usukani. Mara baada ya kuliacha handaki hilo, akapita barabara ndogo ndogo za mitaani, na kuibukia pembezoni mwa jiji hilo.

“Hema ya mkutano?” Amata akauliza.

“Ndiyo, Carmo Convent...” Scoba akamjibu huku akiingiza gari kwenye lango dogo la kutosha wao tu. Akaendesha taratibu kuufuata ushoroba huo wenye giza, uliogeuka kuwa makazi ya buibui na popo. Mwisho wakaibukia kwenye veranda ndogo isiyo na kitu chochote. Taa za gari zikammulika Madam S aliyekuwa amesimama kando kidogo. Amata akamtambua Chiba, TSA 2. Naye alikuwa kasimama hapo na ubamba wake mkononi.

“Karibuni katika Convent ya Carmo...!” Madam S akawaambia Scoba na Amata wakati wakiteremka katika gari hilo. Buti likafunguliwa, Mwanachia akaonekana akiwa amejikunyata ndani yake.

“Umejikunja kama ulivyokuwa tumboni mwa mama yako, mwanaharamu mkubwa!” Madam S akamwambia kwa gadhabu akiwa na bastola mkononi. “Mtoeni, mleteni hapa!” akawaamuru.

* * *

Carmo Convent katika jiji la Lisbon ni sehemu ya makumbusho. Gofu hilo la kanisa ni matokeo ya tetemeko kubwa la ardhi lililotikisa jiji hilo mwaka 1755. Tukio hilo la kuogofya lilitokea tarehe 1 ya mwezi Novemba mwaka huo, siku ya jumapili, Wakristu wakiwa wamejaa ndani yake kusherehekea sikukuu ya Watakatifu wote. Pamoja na tetemeko hilo kuwa kubwa, ni paa tu lililoezuka lakini kuta zake zipo hadi leo. Nchi hiyo imelifanya kuwa eneo la makumbusho ya kihistoria.

Ndani ya gofu hili, mengi hutukia, watu hutumia kwa sherehe, mafunzo, mikutano na mambo mengine ya kijamii. Ni sehemu ya chini ya jengo hili ambako daima hakutumiki, na wapo ambao hata hawakujua kama kuna vyumba au nyumba chini ya jengo hilo. Madam S na Chiba, baada ya kutafiti wapi pa kutimizia kazi yao, walipachagua. Ni Chiba aliyeweka vifaa vyake vya kielektroniki kuhakikisha hilo linawezekana. Kumwongoza Scoba mpaka eneo hilo.

Timu yote ya TSA ilikuwa imetimia ndani ya jengo hilo. Gina akavuta kiti kimoja cha chuma, kikuukuu kilichokuwa eneo hilo. Amata akamkalisha juu ya kiti hicho.

“Za mwizi arobaini, hata kama zikija baada ya miaka mia...” Madam S akamwambia Mwanachia, “mvueni nguo zote!” akaamuru.

“Hah!”Mwanachia akatoa sauti na kuinua uso uliojaa damu. Akafumbua macho na kumtazama mwanamama huyo anayeamuru avuliwe nguo.

“Safi, nilitaka tutazamane, nilifikiri umelala au umezimia... Vincent Mwanachia, mpiganaji mahiri ambaye Afrika na Tanzania tunajivunia kuwa naye. Ukaamua kuasi jeshi lako tukufu, ukadiriki kushiriki uasi mwaka 1980 kwa mara ya pili. Nini hasa lilikuwa lengo lenu? Tunajua kuwa mlikuwa mnataka kulikomboa taifa lenu dhidi ya makucha ya siasa za Mashariki za Ujamaa na kujitegemea... kwa nini mlilikimbia taifa lenu baada ya kushindwa?” Madam S akamuuliza mateka wake aliyekuwa akihema kwa shida.

Hakujibu kitu, badala yake alikuwa na kitu kama kwikwi kikimjia mara kwa mara. Macho yake madogo yalimtazama mwanamama huyo aliyekuwa mita mbili kutoka pale.

“Kamwe hamtoweza kufisha juhudi...” akajibu kwa mkato huku akirudisha uso wake chini.

“Nani aliyekwambia? Nataka unambie wako wapi washirika wako waliobaki?” akamtupia swali.

“Aha ha ha ha haaaaa! A ha ha ha haaaaa!” Mwanachia akaanua kicheko kilichofanya mwangwi wa kutisha. Popo wakatoka katika maficho yao na kuruka huku na huko.

“Achana na sisi wewe malaya uliyekosa kizazi...!” Mwanachia akamwambia Madam S.

Kutoka pale aliposimama, Selina alifyatuka mithiri ya Shaolin, teke moja zito likatua shavuni mwa Mwanachia, akaenda chini mzima mzima. Madam S akaanza kumfuata pale chini, Kamanda Amata akamuwahi na kumvuta nyuma.

“Aaaaaakkkkhhhhh, mwanamke mpumbavu, aaaaaaakkkhhhhh!” Mwanachia akaugulia pale chini. Kwa jinsi alivyokuwa akiongea ilikuwa dhahiri shahiri kuwa amepata maumivu makali katika taya lake.

“Rudia tena nikuue mwanaharamu wewe!” Madam S akang’aka kwa hasira. Mwanachia akaketishwa tena kitini.

“Wako wapi washirika wako?” safari hii swali likatoka kwa Kamanda Amata, akiwa na mkasi mkali mkononi aliyouchukua katika mkoba wa daktari Jasmini sekunde chache baada ya kumuacha Madam S.

“Wewe ni nani uniulize swali kama hilo?” Mwanachia akajibu kwa swali tena kijeuri.

“Majibu ya ‘Yesu’ kwangu huwa hayana nafasi!” Amata akamwambia, ma kumkamata kichwa, akaupachika mkasi sikioni, akasukuma vidole vyake na kuanza kulikata sikio. Damu ikaanza kumwagika.

“Aaaaaaiiiiiiyyyyaaa..... nasema nasema nasema!” akapiga kelele. Amata akalegeza mkono, tayari nusu ya sikio ilikuwa ikining’inia.

“Sema, wako wapi?”

“Rua Camarante, lote 25, aaaaaaiiiiii minha orelha minha orelha,” akaeleza kwa taabu huku akigugumia maumivu. Akawataji mtaa na namba ya kitalu. Wakati hayo yakiendelea mara vikasikika vishindo vya watu wakiteremka ngazi kuja chini ya jengo hilo. Amata akawapa ishara wenzake. Sekunde tatu zilikuwa nyingi sana, wakajificha gizani na kumwacha Mwanachia peke yake pale kitini.

Mara watu wanne wakaingia wakiwa na bunduki mikononi mwao. Wakajipanga mduara, wakimweka Mwanachia kati. Watu wale walikuwa wamevalia nuo nyeusi tupu na nyuso zao zilifichwa kwa barakoa.

“Camarada. você está seguro agora…” mmoja wao akamwakikishia usalama.

“Nós não ... estamos seguros,” akawaambia kuwa hawako salama.

Alipomaliza tu kusema hayo, akajishika paji la uso na kukodoa macho, taratibu akaenda chini mpaka sakafuni na kutua kama mzigo. Risasi ndogo ilididimia katika paji lake la uso na kuishia ndani ya kichwa chake. Yule bwana akamuwahi pale chini.

“Camarada! Camaradaaaaa!” akaita. Akamtikisa. Hakutikisika. “Foi morto, aaaaaaaaaah! Watalipa kifo hiki,” akawaambia wenzake kuwa, ameuawa. Shabaha ya Kamanda Amata kutoka mafichoni ilihitimisha maisha ya mpiganaji muasi, Vincent Mwanachia, akiwa wa pili kwenye orodha aliyopewa na bosi wake iliyomtaka kuwaua.

Wale jamaa wakatawanyika ndani ya lile jengo wakitafuta huku na kule, wasione mtu. Madam S na jeshi lake tayari walikuwa nje, ndani ya gari wakielekea katika maficho yao.

* * *

Taarifa za kuuawa kwa Vincent Mwanachia, zilifika haraka katika moja ya visiwa vya kihistoria katika Bahari ya Hindi. Hapa ndipo bwana mkubwa, mkuu wa sindiketi ile aliweka makazi pamoja na mipango mingine mingi ilisukwa katika kisiwa hiki.

Nje ya jumba kubwa ambalo wengi wao walipenda kuliita Camp Site, aliyekuwa waziri wa zamani wa mambo ya nje, Mr. Mc Tee alijikuta akiangukwa na bilauri ya mvinyo iliyokuwa mikononi mwake. Haraka, akaelekea ndani ya nyumba hiyo na kuteremka ngazi mpaka sakafu ya chini. Akafungua moja ya chumba vidogo vilivyojenwa huko na kuingia kwenye boti. Boti hii ndogo iliweza kupita chini kwa chini kama nyambizi za kivita. Akawasha mtambo wake na kuondoka. Daima wafanyakazi wake walijua kuwa akiingia katika chumba hicho huwa ofisini.

Safari yake iliishia katika kisiwa kingine, umbali wa kilomita mbili hivi. Nako, vivyo hivyo, chombo kile kilisimama chini ya bahari, kisha kikapanda juu taratibu na kutokea katika uwa mpana wa nyumba. Kibwana akateremka na kulakiwa na vijana wake kama sita hivi waliokuwa wakiishi humo.

“Andaeni mazingira kesho kikao cha Sindiketi kitakuwa hapa!” akawaambia huku akiingia ndani ya nyumba hivyo.

“Karibu mpenzi!” Akakaribishwa na mwaDanada wa Kihindi, mwenye nywele mpaka kiunoni. Weupe wake haukuwa hata na tone la chunuzi mintarafu kipele. Alikuwa ndani ya vazi mwororo, la hariri, jepesi lililomuonesha wazi maungo yake. Mwanamke huyu alikuwa hapa kwa kazi moja tu, kumfurahisha kimahaba mwanaume huyu.

Kibwana hakujibu neno, aliongoza mpaka chumba kingine, akaingia na kujifungia, akimwacha yule mwanamke katika sebule ndogo. Hassna, msichana wa miaka ishirini na sita tu, mwenye asili ya Kihindi upande wa mama na Mndengereko kwa baba, alijikuta akiwa mfanyakazi wa ndani katika camp hiyo. Akisafisha vyumba vya watalii wajao hapo na wageni wengine. Bosi akampenda kwa ukarimu wake, akataka binti huyo ahamishiwe kwenye nyumba hiyo iliyo mbali kidogo na camp za wageni. Kwa kuahidiwa pesa nzuri ya kila mwezi, akakubali na kujikuta ndani ya kifungo hasichotarajia. Mke bila ndoa, mpenzi pasi na makubaliano, mama bila watoto. Hakuwa na budi kukubali yote haya pale alipotishiwa kuuawa endapo angekataa kuwa kiburudisho. Ukimtazama anavutia, kiuno chembamba, makalio makubwa kiasi, yanashikika. Kifua chenye matiti kama mapapai machanga, na chuchu kali zenye kuchoma kila amkumbatiaye.

Ndani ya chumba hiki, kulikuwa na meza moja, kompyuta kubwa na kitabu cha kumbukumbu juu yake. Hakukuwa na kiti kingine. Akaketi na kuiwasha ile kompyuta mbele yake. Kisha akachukua kifaa cha kusikilizia akakipachika kichwani mwake mpaka masikioni.

“Lisbon is down!” akasikika akisema. Mc Tee akatulia kimya kwa jozi la sekunde akisikiliza ujumbe wa upande wa pili.

“Bado nashindwa kujua hasa ni jinsi gani wanaweza kutembea juu ya nyayo zetu?” akasikika akisema. Kisha akatulia tena kimya akisikiliza mtu wa upande wa pili. Baada ya dakika kama kumi hivi, akavua kile kidubwasha masikioni mwake na kukipachika kwenye kining’inizio chake. Akaegama kitini na kushusha pumzi ndefu. Baada ya kubofya kitufe fulani, mlango ukafunguliwa. Hassna akaingia ndani, manukato yaliyomfuata nyuma yalikijaza chumba kile na kukifanya kuwa kama pepo ndogo.

“Karibu malkia wangu. Moyo wangu umesawajika, wahitaji tulizo...” akamwambia.

“Hapa nipo kwa ajili yako, kama utakavyo bwana wangu!” Sauti nyororo ya msichana huyo ikapenya masikioni mwa Mc Tee, mwaDanamu mwenye moyo wa pekee kwa waliomzunguka.

Misaada aliyokuwa akiitoa kwa mashule, hospitali na jamii kwa ujumla ilimfanya ajulikane, apendwe, atukuzwe. Mwekezaji, aliyepewa ekari za kutosha katika Kisiwa cha Mafia, Mashariki mwa Tanzania. Mc Tee akajenga kambi kubwa ya kitalii, yenye kila aina ya burudani kwa wenye nazo. Mapumziko kwa wapendanao, likizo kwa watokao mbali, picnics na vikao mbalimbali vya serikali na taasisi zake vilifanyika hapo.



aliyepewa ekari za kutosha katika Kisiwa cha Mafia, Mashariki mwa Tanzania. Mc Tee akajenga kambi kubwa ya kitalii, yenye kila aina ya burudani kwa wenye nazo. Mapumziko kwa wapendanao, likizo kwa watokao mbali, picnics na vikao mbalimbali vya serikali na taasisi zake vilifanyika hapo.

Nyumba aliyokuwa akiishi Mc Tee ilikuwa kando kidogo ya ile kambi ya kitalii. Hapo alikuwa akiishi peke yake. Waliokuwa wakiingia na kutoka ndani humo ni wafanyakazi tu. Hakuna aliyewahi kumwona na watoto wala mke. Alikuwa kapela. Lakini umriwe haukuendana na hali hiyo, ilishangaza. Wengine wakasema ‘labda mkewe yuko kwao India’ na waliobaki wakadhani mgonjwa. Ni Hassna tu aliyeujua ukweli wa mambo. Akasimama nyuma ya kiti hicho, akaanza kumkandakanda mabegani.

“Unaonekana hauko sawa boss!” Hassna akasema. Mc Tee akaishika mikono ya msichana huyo na kumvuta chini kidogo. Shingo zao zikakutana, wakatazamana kwa pembe.

“Kuna jambo limenivuruga,” akamjibu.

“Pole, nipo kwa ajili yako kama utakavyo,” Hassna akasema.

“Ndo maana nilikuchagua kuwa mfariji wangu. Unajua wakati gani unifanyie nini...” Mc Tee akamwambia Hassna, akamvuta kwa mbele na ndimi zao zikakutana. Chumba hakikuwa kikubwa wala hakikutosha kwa kilichoendelea kwa kuwa hakikuwa maalumu. Mkutano wa miili ya wawili hawa ukawa wa burudani zote, harufu nzuriilitawanyika kila Hassna alipoongeza manjonjo katika mtanange huo. Dakika arobaini na tano ziliwaacha hoi, kila mmoja akihema kama mbwa, vinywa wazi. Hassna bado alitamani kuendelea lakini Mc Tee alikuwa nyng’anyang’a. Simu ya mezani ikaita kwa fujo, akamwacha mwanamke huyo na kuinyakua.

“Yes Comrade!” akaitikia kwa kuwa alijua ni wapi simu hiyo inatoka.

“...sawa gati namba mbili ni salama!” akajibu na kukata simu. Akamtazama Hassna, kisha akarudisha macho kwenye ile kompyuta.

“Kesho kuna kikao, weka kile chumba tayari na vile vya wageni vyote viwe katika hali ya usafi...” akamwambia.

* * *

Siku hiyo hiyo, ndani ya jumba kubwa lililojengwa pembezoni mwa ufukwe wa Tamariz katika kijiji cha Cascais, Mghalibi mwa jiji la Lisbon, TSA walikutana. Kutokana na usiri wa kazi yao, ni Madam S pekee aliyekuwa akijua kuwa timu hiyo ipo jijini Lisbon. Kila mmoja alitumwa kwa kazi yake na aliifanya kwa weledi wote. Kamanda Amata na Madam S walikuwa wa mwisho kuwasili katika jiji hilo. Mikononi mwa wote, mlikuwa na kazi moja tu iliyofumbwa kwao isipokuwa Amata. Yeye alijuwa wazi kuwa anakwenda kuitoa roho ya Vincent Mwanachia.

Walikuwa ndani ya chumba kidogo, kila mmoja akiwa amemaliza kazi yake kiukamilifu. Ukimya ulitawala, hata sindano ingeanguka, basi ingesikika kiurahisi sana. Gina alikuwa akimtazama Amata kwa jicho pembe, lakini hakusema lolote.

Katika tukio hili mambo yalikuwa tofauti kabisa, ukilinganisha na lile la Ubelgiji. Na hili ndilo lilifanya Madam S awakutanishe wote katika pango lile kongwe la Carmo Convent.

“Sikutaka iwe hivi, lakini kaka yenu amefanya iwe hivyo...” Madam S akawaambia vijana wake, kisha akatulia kwa jozi la sekunde.

“Wakati mwingine inabidi, ili kuhakikisha usalama wa ninyi nyote. Hatuna muda wa kupopteza sasa, tumeshamwondoa ayawani wa pili, hao wengine tutajipanga tufanyeje!” Madam akaeleza, “cha muhimu kwa sasa ni kila mtu kuondoka, tutaonana Dar es salaam,” akaogeza kusema.

Muda wote ambao Madam S alikuwa akiongea, chumba kile kilitawaliwa na ukimya wa kuogofya. Ubongo wa kila mtu ulikuwa ukitafakari tukio lililopita usiku huo.

“Dana na mkuu wake lazima washughulikiwe, walitaka kutuingiza chaka,” Amata akasema.

“Hilo halina shaka,” Madam akamjibu.

Baada ya mazungumzo machache, wakatawanyika, kila mmoja akiwa na jambo moja tu mbele yake, kufika Dar es salaam.

Dakika zilizofuatia, ndani ya chumba kile alibaki Kamanda Amata na Madam S pekee.

“Hongera Kamanda, akili uliyoitumia leo, imeokoa mengi sana katika upande wetu,” Madam S akamwambia Amata.

“Ilibidi nicheze plani B. Na nina uhakika kilichotokea leo, kitawafanya wajifikirie uzembe walifanya wapi,” Amata akajibu.

“Sure! Sure! Sasa kibarua ni hiki kinachotukabili... bado watatu, Marehemu Kibwana Mtokambali... lazima tujue kazikwa wapi. James Msambamagoya na Jesca Tibatulanwa,” akamwambia.

“Kuwapata hawa ni kazi nzito maana hata fununu hatuna,” Amata akasema.

“Watapatikana tu, TSA si idara ya kuchezea ...”

“Hakika...” Amata akamalizia kwa jibu fupi. “Usiku huu, lazima nifike Rua Camarante, lote 25, kama alivyosema mwenyewe Mwanachia,” Amata akaeleza.

“No Kamanda, achana na hilo, huwezi kujua isije kuwa mtego,” Madam S akaingiwa na woa na kumwonya Amata.

“Kumbuka swali tulilomuuliza, kabla hajafa akajibu namna hii... inatubidi twende. Hatari na vifo ndiyo sehemu ya maisha tuliyoichagua, kwa nini tuogope?”Amata akamuuliza bosi wake.

“Ok ninaheshimu mawazo yako. Kumbe Gina angebaki kukusaidia maana najua unaweza jikuta msambweni,” akasema Madam S.

“Ni kweli, ila angenitia uvivu, nitalishughulikia mwenyewe... naamini sintoiacha roho yangu ugenini...” Amata akasema huku tayari akiwa ameinuka. Madam S akamtazama kutokea pale alipoketi, akambania jicho la kulia.

“All te best kijana! Taifa linakutegemea,” Madam akamwambia, kisha akamshuhudia Amata akipotelea nje ya ile nyumba ndogo iliyojengwa kando tu ya ufukwe wa Tamariz.

* * *


Rua Camarante, lote 25


Kamanda Amata alipita kwa mwendo wa taratibu katika barabara hiyo akichunguza vibao vinavyoonesha namba za viwanja. Haikumuwia ngumu kukiona kile anachokihitaji. Kitalu namba 25. Akatikisa kichwa kuwa ndicho haswa. Kwa mwendo uleule, akaendelea kuifuata barabara ile mpaka upande wa pili. Katika barabara ile, kulikuwa na baa mgahawa wa kisasa uliojitambulisha kwa harufuza vyakula.

Amata akaegesha gari katika mgahawa huo, akateremka na kuliacha hapo. Akavuka barabara, na kwa hatua za wastani akatembea kurudi na ile barabara mpaka alipoifikia ile nyumba. Akachukua kama dakika mbili hivi kama si tatu kuchunguza usalama wake. Alipojiridhisha na usalama wa nyumba hiyo, ilimchukua sekunde tatu kuuruka ukuta na kutua ndani bila klufanya kishindo. Sekunde nyingine tano zikamfikisha kwenye mlango wa barazani. Akatembeza macho yake katika maua yaliyopandwa eneo hilo. Japo hakutaona vyema kutokana na giza la usiku huo, kiukweli alikuwa akiangalia kitu kingine kabisa. Hisia zake zilipomruhusu, akapachika ufunguo wake na kufungua mlango huo pasi na kipingamizi. Akakaribishwa na sebule ya wastani yenye viti vinne tu, na juu ya meza ndogo iliyozungukwa na viti hivyo, kulikuwa na klibweta cha jivu la sigara. Yote haya aliyaona kwa miwani yake maalumu yenye uwezo wa kuona gizani. Alipoambaza macho ukutani, alikutana na picha moja ya watu watano. Wawili kati yao walivalia mavazi ya kijeshi. Mmoja wao alikuwa mwanamke. Picha hii ilivutia macho ya Amata, akaisogelea. Hakuiacha. Baada ya kuichukua, akaendelea na safari yake kwa kupita chumba kimoja baada ya kingine. Ni kwenye chumba cha mwisho ndipo alipopata anachofikiri. Kompyuta, laptop, ilikuwa mezani. Pembeni ya meza hiyo kulikuwa na kitanda kilichovurugika kana kwamba kulikuwa na watu waliokuwa wakikitumia. Hilo halikumvuta. Kompyuta, hiyo ndiyo iliufurahisha moyo wake. Hakuibeba, aliigeuza kwa mikono yake yenye glovu nzito za ngozi. Kwa vifaa vyake, akaipachua Hard Disc na kuitia mfukoni.

Alipokuwa akitaka kutoka, akasikia muungurumo wa gari, mara geti likafunguka. Amata akatoka haraka na kujificha kwenye chumba cha pili.mlango wa chumba hicho akauacha wazi kidogo sana ili tu aone nini na nani wapo ndani humo.

“Kama tutaikuta itakuwa heri sana!” sauti ya kiume ilisikika wakati mlango ukifunguliwa.

“Lazima iwepo, tuliiacha baada ya kumaliza kazi yetu, na alisema atakuja aichukue ili aipeleke...” sauti ya kike ikajibu. Wakapita na kufungua kile chumba, wakaingia.

“Oh, Thank God! Hii hapa,” yule jamaa akasema. Amata akawaona wakitoka tena, mkononi mwa yule kijana alikuwa na ile kompyuta.

Nimewawahi! Amata akawaza huku akiwang’ong’a. Akawaacha waende. Aliposikia muungurumo wa gali likiondoka, na yeye akajitokeza na kutembea haraka haraka. Kwa njia ileile aliyoingilia ndipo akatokea na kupotelea gizani.




DAR ES SALAAM


1981


NDANI YA OFISI YAKE YA SIRI, Chameleone, alipokea taarifa za kutoweka kwa Waziri Kibwana Mtokambali. Haikumuingia akilini hata kidogo. Akaona, kuna haja ya kufanya haraka kuwatia mbaroni wote waliohusika na njama hiyo. Akavuta droo ya meza yake na kuchukua ile karatasi, akatazama orodha nzima. Kisha akaangalia na orodha nyingine ambayo aliipata kupitia watu wake wa siri, aliowapa kazi hiyo.

“Swadakta!” Akajisemea.

Kwa kutumia simu yake ya mezani, akatoa amri ya kukamatwa wote ambao wameorodheshwa katika karatasi hizo mbili. Mshike mshike ukaanza, kambi kwa kambi, nyumba kwa nyumba. Wengi wakatiwa mbaroni. Waliohusika kwa namna yoyote ile, walikamatwa.

Kwa saa kadhaa, hakutoka pale ofisini, alikuwa akisubiri apate taarifa ya nani na nani wapo katika mikono ya dola. Kufikia jioni ya siku hiyo, akiwa ameshapanga mipango yake vizuri, simu ya mezani ikaita. Akainyakuwa na kuiweka sikioni.

“Hallo!” Akaita.

“Hallo... pokea taarifa nzito kama ifuatavyo,”sauti ya upande wa pili ikamwambia.

“Mia!” Akajibu, akiwa na maana ya kumruhusu aendelee. Kutoka upande wa pili akapatiwa majina ya watu wote waliotiwa mbaroni katika operesheni ile.

“Katika orodha ya kwanza hatujaweza kuona hata nyanyo...”

“Kati ya zote?”

“Ndiyo!”

Taarifa hii haikumpa furaha Chameleone. Kwa upande wake alipenda hao ‘papa’ wakamatwe kwanza maana ndiyo wasuka mipango. Mara hii akanyanyuka kutoka kitini, akachukua miwani yake na kuipachika usoni. Akatoka katika ofisi hiyo na kuingia katika gari lake, Land Rover 109. Akalitia moto na kuondoka zake.

Haikumchukua muda mrefu, akaingia katika viwanja vya Ikulu, Magogoni. Kila aliyekutana naye alikuwa katika hali isiyo ya kawaida. Zaidi ya kusalimiana kwa kupungiana mikono, hakuna lililoongelewa. Akazikwea ngazi na kupotelea ndani ya jengo hilo jeupe. Breki ya kwanza ikawa katika ofisi ya Makamu wa Rais. Akamkuta. Mzee huyo alitamani kumrukia Chameleone. Alisimama haraka na kukiacha kiti chake, akavuta hatua kama tatu hivi na kumfikia mwanausalama huyo.

“Afadhali umefika. Kuna mambo tata hapa, tumeshindwa kuyapatia ufumbuzi,” akamwambia.

“Usiwe na wasiwasi mkuu, vijana wapo kazini, kila lenye utata litatatuliwa,” Chameleone akajibu huku akivuta kiti kukaa na Makamu wa Rais akafanya vivyo hivyo.

“Nchi imekuwa kimya, napokea simu kutoka kwa majirani wanauliza kuhusu Mheshimiwa Rais, wao wanajua tumepinduliwa,” Makamu akaeleza.

“Ukawajibu nini?”

“Nimewaambia tu watulie, maadam mimi ndiye ninayeongea basi nchi haijapinduliwa”.

“Ni sahihi, nchi ipo salama, na Rais yupo salama kabisa. Naamini jioni ya leo atalihutubia taifa,” Chameleone akasema. Mara hiyo hiyo, mlango ukafunguliwa, msichana mbichi mwenye umbo la kuvutia, akaingia ndani. Nywele zake ndefu zilizochanwa Afro, ziliudhihirisha ulimbwende wake. Sketi yake ya mtindo wa Zembwela ilimkaa vyema mwilini. Akasimama kando, kwa heshima zote, akakabidhi faili moja kwa Chameleone.

“Asante Selina, nipatie taarifa yako kwa kifupi,” akamwambia.

“Operesheni imekamilika kwa asilimia themanini. Tumewatia mbaroni watu wapatao ishirini na tatu. Wote hao wamehifadhiwa katika Gereza la Ukonga kusubiri utaratibu mwingine wa mahojiano. Lakini watu watano, wenye vyeo vya juu, ambao imesadikiwa ndiyo wasuka mipango, wametoweka kabisa. Kwa tafiti zetu mpaka sasa hatujapata fununu yoyote, na upelelezi unaendelea. Hayo tu,” Selina akamaliza kuwasilisha taarifa hiyo.

“Asante kaendelee na kazi,” Chameleone, akamjibu na kumruhusu kuondoka. Akamgeukia tena Makamu wa Rais na kumsukumia kabrasha lile. Alipolipokea akamwambia, “sitaki kuamini kabisa kama Waziri Mtokambali ni mmojawapo”.

“Kikulacho, ki nguoni mwako mheshimiwa. Tegemea kumpokea Rais muda wowote kutoka sasa,” akamwambia na kusimama, wakaagana.



KIGAMBONI


Katika nyumba pweke aliyokuwa amehifadhiwa Mkuu wa nchi, hakukutokea lolote la kuhatarisha maisha yake. Yeye alikuwa akifuatilia kila kitu kupitia redio ndogo aliyokuwa ameachiwa na mlinzi wake. Punde si punde, akasikia muungurumo wa gari likisimama nje ya nyumba hiyo. Akatulia kusubiri kuona nini kitajiri. Haikusikika sauti ya mtu yeyote kuongea isipokuwa hatua tu za mtu anayetembea haraka haraka.

Mlango ukafunguliwa, mtu huyo akaingia ndani mpaka kwenye kile chumba.

“Mkuu, natumaini u mzima!” Akasema Chameleone.

“Bukheri wa afya. Nilikuwa naendelea kufuatilia taarifa mbalimbali hapa za ndani na nje ya nchi kwa redio hii. Dunia inasadiki kuwa tumepinduliwa...”

“Ni kweli, lakini sasa ni wakati wa kuishangaza pia. Nimekufuata, nikurudishe Ikulu, ukaendelee na majukumu yako. Watanzania wanaisubiri sauti yako kwa hamu sana. Wamekuwa kama vifaranga vilivyonyeshewa na havimuoni mama yao,” Chameleone akamkatisha kwa sentensi yake. Baada ya mazungumzo mafupi wakatoka pamoja na kuingia kwenye gari. Tayari ilitimu saa kumi jioni, walipoondoka na kuiacha nyumba hiyo.

Jambo alilolifanya mwanausalama huyu, ni kumfikisha Rais, kwanza katika ofisi yake ya siri. Akampa taarifa yote ya kazi inayoendelea. Pia akamweleza na wale waliotoroka.

“Hata wakitoroka, kesi yao itakuwa palepale na sheria itawashughulikia maadam hawajatorokea sayari nyingine,” Rais akasema. Kishapo, akamchukua na kumpitisha mlango wa nyuma, mjia za siri mpaka katika jengo la Ikulu. Akaingia naye ndani mpaka katika ofisi yake. Wafanyakazi waliokuwa katika mfadhaiko mkubwa, walipomwona, wapo waliotamani kupiga vigeregere, wengine hata kumbeba.

Taarifa ya kurudi kwa Rais Ikulu, ikasambaa kama moshi wa kifuu. Akapokelewa na makamu wake, Waziri wa Ulinzi na wa Mambo ya ndani. Wanausalama nao wakachukua nafasi zao kumuwekea ulinzi mkuu wa nchi.

Ndani ya ofisi ya Rais, ilikuwa ni kupokea taarifa tu za sakati zima. Saa moja usiku ya siku hiyo hiyo, mafundi wa Redio Tanzania walikuwa pale na OB Van lao, tayari kurusha hotuba ya Rais mubashara. Katika chumba maalumu kilichoandaliwa kwa shughuli hiyo, wanahabari, pamoja na wanausalama, walikuwa kimya kusubiri nini kitaendelea. Katika hali ya kushangaza hawakuamini walipomwona Rais yuleyule ambaye alitoweka kwa saa kadhaa na watu kujua kuwa ameuawa. Makofi ya shangwe yakasikika na kukijaza chumba kizima.

Hotuba ya kusisimua ikawafikia Watanzania popote walipo. Hoi hoi na nderemo zikasikika kila kona ya nchi. Akinamama wakaimba, akina baba wakapiga ngoma, ili mradi ni furaha. Waliotaka mapinduzi wakabaki vinywa wazi, hawana la kusema. Aibu ikawapata popote walipo. Nchi ikatulia, maisha yakaendelea.


Majuma matatu baadae...

Katika Mahakama Kuu, kesi ya uhaini ikaunguruma. Nani yumo na nani hayumo, upelelezi ulikuwa ukiendelea. Wengine wakaachwa huru na wengine wakapata kifungo cha maisha jela. Watano kati ya wote waliotajwa katika kesi hiyo hawakuwepo maakamani na wala haikufahamika wapi walipo. Wamekufa au wapo hai. Utata.

Kwa upande wa mahakama hilo halikuzuia kitu. Jaji aliyekuwa anaendesha kesi hiyo alisoma hukumu ya dakika arobaini na tano. Akawahukumu kifo watu hao watano akiwataja kwa majina; aliyekuwa mkuu wa kikosi cha Jeshi la Anga Titus Mwakibinga, aliyekuwa mkuu wa kambi ya Twalipo, Vincent Mwanachia, aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje, Kibwana Mtokambali na James James Msambamagoya, mwanausalama namba mbili wa Rais. Mahakama ikafungwa.

Mara baada ya sakata hilo, Rais akaifumua idara ya Usalama wa Taifa na kupanga upya safu yake. Pamoja nayo ikaanzishwa falsafa ya ‘kila mwananchi ni mlinzi wa taifa lake’. Hatua nyingine ikachukuliwa, wakatengenezwa mapandikizi na kupandikizwa kila Nyanja iwe ya kiserikali au binafsi. Yote , ili kupata habari yoyote hata iwe ndogo kiasi gani. Ikafanikiwa.

* * *



MAKAO MAKUU YA T.S.A MARCH 1999


Juu ya meza kubwa anayoitumia Madam S, palikuwa na bahasha moja ya khaki iliyopigwa mhuri uliosomeka ‘CONFIDENCIAL’. Asubuhi hii mara tu baada ya kupata kifungua kinywa, aliichukua bahasha hiyo na kuichana ili kupata kujua nini hasa kipo ndani yake.

‘Ionwe na mhusika tu’ ilianza kwa kuandikwa namna hiyo. Baada ya anwani za serikali na protokalizote za uandishi wa barua kukamilika. Iliendelea.

HATI YA KIFO

…watafutwe popote walipo, wauawe.

Chini yake kukawekwa orodha ya majina manne. Moja kwa moja , Madam S aliukumbuka mkasa huu. Akaendelea kusoma maelezo mengine na kisha akakutana na picha nne za watu hao. Lakini mstari wa mwisho ulidhihirisha wazi kuwa hakuna taarifa yoyote ya wapi watu hao wanapatikana. Na waraka huo ukaeleza kinagaubaga kuwa kuna mapandikizi ya watu hao ndani ya Tanzania, wakifuatilia nyendo na kupata habari zote juu yao. Hata mwanausalama aliyeteuliwa na TNS kufuatilia kujua watu hao wako wapi, alipotea katika mazingira ya kutatanisha mwaka 1990.

Madam S, akaikunja ile karatasi na kuitia kwenye droo.

Limenirudia mwenyewe, sikutegemea kama tutafukua makaburi! Akawaza. Akajiegemeza kitini, kimya. Tayari akili na mawazo yake vikatekwa na maandishi hayo. Saini iliyohitimisha waraka huo ikampa kigugumizi cha kuamua. Tangu litokee sakata la kujaribu kupindua serikali ni miaka kumi na nane ilikuwa imepita. Awamu ya tatu ya utawala, ilikuwa inakaribia kuingia kipindi chake cha pili. Akatafakari kwa jozi la dakika. Aanzie wapi, aishie wapi. Akamkumbuka mwanausalama huyo kijana aliyetoweka, kwa jina moja tu la Dastan. Lakini hakuwahi kujua kama mtu huyo alikuwa kwenye kufuatilia sakata hilo hilo.

Serikali na siri zake! Akawaza.

Naanzia wapi? Akajiuliza. Kila alipoitazama karatasi ile, ilikuwa kana kwamba inamwambia ‘anza sasa’. Madam S akasimama akageukia upande wa nyuma. Macho yake yakatazama nembo kubwa ya TSA iliyonakshiwa kwa nyota sita na kuzungukwa na maandishi, ‘For my people. For my nation’, ikiwa ni sehemu ya kiapo chao, ‘Kwa watu wangu. Kwa taifa langu’. Akapiga saluti, akaketi tena kitini. Akainua mkonga wa simu na kukoroga tarakimu kadhaa.




Macho yake yakatazama nembo kubwa ya TSA iliyonakshiwa kwa nyota sita na kuzungukwa na maandishi, ‘For my people. For my nation’, ikiwa ni sehemu ya kiapo chao, ‘Kwa watu wangu. Kwa taifa langu’. Akapiga saluti, akaketi tena kitini. Akainua mkonga wa simu na kukoroga tarakimu kadhaa.


* * *

Upande wa pili, simu ile ilifikia katika kijimeza kidogo kando ya kitanda kikubwa cha futi tano kwa sita. Kwa uchovu aliokuwa nao, Kamanda Amata akaipuuzia. Hakuijali. Dakika mbili baadae, ikaita tena na kukatika, kasha ikaita kwa mara ya tatu. Akageuka haraka, Danani ya shuka na kuinyakua. Kwa kuwa ilikuwa haina waya, akarudi nayo katikati ya kitanda.

“TSA 1,” akaitikia.

“Unakoroma tu mwanaume…”

“Sasa nifanye nini! Na ndiyo kwanza likizo ipo siku ya pili…”

“Hah! Hah! Hah! Hah! Na ndiyo imesitishwa kwa taarifa yako…” Madam S akacheka na kumwambia Amata, “tukutane Saint Albano nusu saa ijayo”.

Amata akakunja sura kwakukatishwa usingizi wake. Akajivuta kivivuvivu na kuketi, kasha akapia mwayo mrefu na kunyoosha mikono yake; huu upande ule na mwingine ule kule.

Hizi kazi zingine hizi majanga tu, sijui kuna nini tena! Akawaza huku akinyanyuka na kuelekea maliwato. Dakika ishirini baadae akawa jikoni akitengeneza staftahi nyepesi kwa ajili yake. Kahawa ya Kiitaliano, slesi nne za mkate uliopakwa jam, siagi na asali kidogo na ndizi mbivu. Alipojiweka sawa akachukua pikipiki yake kubwa ya Kirusi, Cagiva, tayari kwa safari. Katika jiji la Dar es salaam, ili uwahi miadi, tumia aina hii ya usafiri.

* * *

Kanisa la Anglikana, lililojulikana kama Saint Albano, lilikuwa pembezoni tu mwa Barabara ya Azikiwe karibu kabisa na Posta Mpya. Madam S aliwasili mahali hapo dakika nne tu kabla ya muda wa miadi. Moja kwa moja akaingia katika duka la vitabu na kupitia rafu zilizobeba vitabu mbalimbali. Dakika tatu baadae, Kamanda Amata , naye aliingia katika duka lilo hilo. Moja kwa moja akaelekea katika rafu ambayo Madam S alikuwapo.

“Mama!” akaita kwa sauti ya chini. Madam S akageuka, si kwamba hakumuona, la, bali alitaka kuonesha luwa hawajaonana siku nyingi ili kupoteza mitazamo ya waliomo ndani.

“Oooh mwanangu!” akaitika na kumkumbatia. Kasha wakachukua kama dakika mbili za maamkio hayo. Na baada ya hapo wakatoka mpaka nje ya duka hilo na kuingia katika mgahawa mdogo, wakaketi humo.

“Asubuhi sana Madam!” Amata akamwambia.

“Najua, taarifa inayokuja asubuhi ina mambo yake mwanangu. Niliopna nikikwambia wakati ule ungeweza hata kupoteza fahamu. Lakini taarifa iliyonifikia ni kwamba, mama yako ni mgonjwa na anahitaji msaada wa haraka,” Madam S akamwambia.

“Oh! Anaumwa tena?” Amata akauliza.

“Ndiyo, hali yake imerudi tena kama siku zote, wewe kama mwanawe wa kwanza, anakutegemea sana, tena sana aisee,” Madam S akamwambia. Kisha akatia mkono mfukoni na kuchomoa bahasha ndogo, akampatia. Madam S, akainuka kitini na kuondoka bila kuaga. Amata akamsindikiza kwa macho mpaka alipopotelea katika lango kuu. Akarudisha macho yake kwenye ile bahasha, akaifungua taratibu na kutoa karatasi ndogo ndani yake. Haikuwa na maneno mengi. Macho yake yakagongana na kifungu cha Biblia na maneno machachhe.

‘Rafu namba tano, biblia ya sita kutoka kushoto. Soma, Ezekieli 33:8-9’.

Amata akatulia kimya kwa jozi la sekunde. Hakuelewa nini maana ya maneno hayo. Akainuka taratibu na kurudi mpaka katika duka la vitabu. Mara baada ya kuingia, akaifuata rafu hiyo. Akahesabu mpaka ile Biblia aliyoelekezwa na kuichukua.

Moja kwa moja akafungua kitabu cha Ezekieli sura ile ya telathini na tatu, aya ya nane mpaka ile ya tisa. Ikasomeka…


8 Nikimwambia mtu mwovu:

‘Wewe mtu mwovu hakika utakufa’;

lakini wewe husemi chochote ili kumwonya yule mtu mwovu aachane na mwenendo wake; mtu huyo hakika atakufa kwa kosa lake; walakini nitakudai wewe kifo chake. 9Lakini ukimwonya mwovu aachane na mwenendo wake, naye haachani na mwenendo wake mbaya, yeye atakufa kwa kosa lake; lakini wewe utakuwa umeyaokoa maisha yako.

Kifungu hicho cha maandiko kilisomeka namna hiyo. Baadhi ya maneno yake yalikuwa yamepiiwa mstari kwa wino mwekundu. Kamanda Amata akajua wazi kuna ujumbe uliofichwa ndani yake ambao hakutakiwa kuupata moja kwa moja kiurahisi tu.

Nikimwambia mtu mwovu: ‘Wewe mtu mwovu hakika utakufa’; hakika atakufa kwa kosa lake; Lakini ukimwonya mwovu aachane na mwenendo wake, naye haachani na mwenendo wake mbaya, yeye atakufa kwa kosa lake;

Kamanda Amata akaunganisha maneno hayo akilini mwake, kitu pekee alichong’amua ni kuwa kuna mtu anayetakiwa kufa. Akashikwa na kibuhuti, akatulia kimya kuiacha akili yake itafakari jambo.

Nani? Akajiuliza. Akiwa katika hali hiyo, simu yake ikafurukuta mfukoni, akaitoa na kufunua ujumbe uliokuwa umefika, namba ya mtumaji ilifichwa.

‘Maktaba kuu ya taifa, kitengo cha NBA, gazeti la Mfanyakazi la terehe 14 June, 1980 ukurasa wa 3’.

Hakupoteza muda, akaachana na duka hilo, akaiendea pikipiki yake na kuiwasha. Dakika mbili tu alikuwa katika uwanja wa Maktaba Kuu, akaingia mpaka kule alikoelekezwa. Akapata huduma aliyokuwa anaihitaji. Akaketi kwa utulivu na kuisoma habari yote kwa makini. Habari hiyo ilikuwa ikihusu kesi ya uhaini na hukumu yake. Aliisoma kwa kuirudia rudia. Ndani ya habari hiyo mwandishi aliainisha mambo matatu katika hukumu iliyotolewa na jaji huyo. Hukumu ilikuwa ni kwa kundi la watu waliojaribu kuipindua serikali ya wakati huo. Kundi hilo liligawanywa mara tatu; kuna walioachiwa huru, waliofungwa maisha na wengine walihukumiwa kifo.

Kamanda Amata akashusha pumzi, sasa akaiona kazi inayomkabiri baada ya aya ya mwisho ya habari hiyo kumwambia kuwa waliohukumiwa kifo wote hawakuwapo mahakamani wala nchini kwa ujumla. Akasonya.

Habari hii alikwishakusimuliwa mara nyini na baba yake wakati akiwa shule ya msingi.

Alikadharika aliisikia vijiweni kwa wengi wanaojifanya wanajua mambo. Hasa kuuawa kwa yule Komandoo ijapokuwa kulikuwa na chumvi nyingi ndani yake ili inoge. Hakuwahi kufikiri , lakini leo hii gazeti lilikuwa mbele yake, alichokuwa akikisoma ndicho alichosimuliwa miaka mingi. Akagundua kuwa hata wale wa vijiweni walikuwa hawasomia magazeti ila porojo tu.

Mambo haya mawili yalimfanya Amata azame kwenye tafakari. Kipande cha maandiko matakatifu na Gazeti la Mfanyakazi.

Halafu nini kinafuata? Akajiuliza. Akainuka na kuwaaga wenyeji wake, akapotelea nje. Akiwa tayari juu ya pikipiki yake, kabla ya kuiwasha, mbele yake akakutana uso kwa uso na kijana aliyekuwa akiuza urembo kwenye kisanduku kidogo.

“Kaka mpende mkeo…” yule kijana akamwambia Amata huku akifungua kile kisanduku chake.

“Sijaoa bado!” Akamjibu.

“Hata kama, lakini kuna vile vinavyompendeza shemeji yangu. Fahari ya macho haifilisi duka kaka…” yule kijana akazidi kupigia debe biashara yake huku akifunua upande wa chini kabisa. Macho ya Amata yakagongana na bahasha ndogo nyeupe, juu yake ilikuwa imeandikwa, ‘ZE SINDIKET’.

“Kwa ajili yako hiyo kaka, chukua chukua,” yule kijana akamwambia Amata. Naye akaichukua ile bahasha na kuitia mfukoni. Akachomoa noti ya silini elfu tano akampatia, kisha yule kijana akaondoka zake. Amata akawasha pikipiki yake na kuondoka. Akaikamata barabara ya Bibi Titi mpaka makutano yake na ile ya Ally Hassan Mwinyi. Akaendelea nayo mpaka karibu na njia panda ya kuingia Agha Khan. Akakunja kulia na kuegesha pikipiki mbele ya Kanisa la Orthodox.

Akashuka na kurudi nyuma hatua kadhaa, akaingia katika uwanja wa makaburi wa mashujaa wa Jumuia ya Madola.

Madam S, alisimama karibu kabisa na uziowa makaburi hayo, akitazama jengo la Hospitali ya Agha Khan na kuipa mgongo barabara ya Ally Hassan Mwinyi. Kamanda Amata akasimama kando yake na kujikohoza.

“Umepata changamoto ya kutosha leo,” Madam S akamwambia bila kumtazama.

“Ndiyo nini kunizungusha hivyo?” Amata akauliza.

“Kila ulipopita, pana ujumbe wa kukupa.”

Amata akanyamaza kimya. Macho yake yakiwa upande uleule ambao Madam S alikuwa akitazama.

“Sawa, nimekuja!” Amata akamwambia Madam huku akiiweka vyema miwani yake ya jua. Madam S akageuka na kumtazama kijana wake.

“Safari hii una kazi tofauti kidogo,” akamwambia, “ulikuwa unaua kwa sababu za kujilinda. Lakini sasa unatakiwa kuua kwa agizo kutoka juu…” akavuta hatua kuelekea mlango mkuu wa uwanja huo huku Amata naye akimfuata. Mbele kidogo, akasimama na kumtazama kijana wake. Wakatazamana.

“Una watu wanne wa kuua, kama ulivyosoma kwenye lile gazeti. Mpaka sasa ni mmoja tu ambaye tumeanza kupata harufu ya wapi alipo, wengine watatu ni kitendawili,” akamwambia.

“Kwa hiyo…”

“Kwa hiyo nini? Tafutishi ikikamilika inabidi ukaondoa roho ya huyo jamaa. Ni utekelezaji wa hukumu yake,” Madam S akasema.

Kamanda Amata akashusha pumzi ndefu, akaweka mikono yake kiunoni huku jicho lake likiwa kwa bosi wake.

“Katika hili hili, kuna jambo linanitatiza sana, lakini ukija ofisini tutaongea. Kaweke begi lako tayari kwa kazi, muda wowote hata kama si leo utatakiwa kuondoka,” akamwambia na kuanza kuvuta hatua ndefu ndefu kuelekea nje ya ule uwanja.

“Na likizo yangu…”

“Utamalizia ukirudi,” akamjibu na kuingia arini tayari kwa safari.

Kamanda Amata akabaki kimya akilitazama gari la Madam S likipotelea mjini. Akaitazama pikipiki yake, kisha akaifuata na kusimama kando yake. Kichwa chake kikazama kwenye lindi la mawazo. Kazi mpya imemfikia.

“ulikuwa unaua kwa sababu za kujilinda. Lakini sasa unatakiwa kuua kwa agizo kutoka juu…”

Sauti ya Madam S ikamrudia kwa mwangwi katika ubongo wake.

Natakiwa kuwa muuaji. Assassin! Akawaza moyoni. Kamanda Amata hakuwa na jingine, zaidi ni kukubali kazi. Kama aliichagua na kuikubali kazi ya Kijasusi basi hakuwa na budi kukubaliana na yote yaliyo ndani yake, maadam tu yanakuwa ndani ya kiapo chake. Akapanda pikipiki yake na kuondoka.

* * *

Jioni ya siku hiyo hiyo, Madam S alipokea nukushi kutoka nchi ya mbali. Na hakika alikuwa akiisubiri hiyo kwa saa nyingi.

‘Kazi imekamilika kwa aslimia sabini na tano,

Tumefanya kila kitu, kilichobaki nikubeba mzigo we tu.

HIvyo waweza tuma lori limalize kazi hii… Omega!’

Nukushi ile iliishia hapo. Yeye Madam S aliielewa vyema kile ilichokuwa ikimwambia. Akaichukua ile karatasi na kuikunja kisha akaitia kwenye droo yake ya mezani. Akavuta simu yake na kupiga tarakimu kadhaa kisha akasubiri.

“Kumekucha, njoo ofisini ukiwa tayari kwa safari,” Madam S akazunumza sentensi hiyo moja tu na kukata simu. Muda uliombakia alikuwa akipa simu huku na kule akiweka vizuri jambo hili na lile. Nusu saa baadae, mlango wa ofisi ukagongwa, Kamanda Amata akaingia.

“Safi sana, umevaa kama mcheza kamali leo,” akamtania.

“Kawaida yangu,” Amata akajibu huku akijikaribisha kitini. Suti ya gharama iliusitiri mwili wake, na kumfanya aonekane haswa, kibopa. “Na ole wako unipe tiketi ya economy, nitarudia hapa hapakuendelea na likizo yangu,” akamwambia.

“Usijali mwanangu!” akamwambia na kumpatia bahasha nyeupe iliyofungwa barabara. Kamanda Amata akaichana, ndani yake akatoa tiketi ya ndege na kadi janja ya Master itakayomwezesha kutoa pesa popote pale duniani. Alipojiridhisha akaitia ndani ya mfuko wa koti. Madam S akampatia bahasha nyingine. Akaichana, ndani yake ikadondoka picha, akaitazama na kuigeuzageuza kisha akachomoa karatasi iliyokuwa ndani yake. Akaisoma.

“Unasubiriwa Brussels, hakuna anayejua safari yako zaidi ya mimi na wewe mwenyewe. Fika pale, ndani ya saa ishirini uwe umemaliza kazi na kurudi hapa,” Madam S akatoa amri.

“Maelezo zaidi…”

“Utayakuta huko huko… Hii ni kazi isiyo na jasho Amata, au siyo?” Madam akamuuliza.

“Itategemea, kwangu mimi hii ni kazi ngumu zaidi kwa sababu natakiwa kumuua mtu asiyenipa upinzani. Nitajaribu,” akasema na kuiweka vyema tai yake, “tutaonana kesho kutwa,” akaaga.

“Kazi njema!” Madam S akaitikia na kumpa mkono wa heri. Amata akatoka nje na kutafuta usafiri kuelekea uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere.


COIMBRA – URENO


ALFAJIRI YA SIKU ILIYOFUATA, Madam S na Kamanda Amata waliwasili katika mji wa

Coimbra, kilomita 210 kwa kupitia mji wa Santarem na Fatima. Moja kwa moja walifika katika uwanja mdogo wa ndege. Dakika sitini na sita ziliwatosha kupata ndege ya kukodi ambayo ingewafikisha katika Jiji la Madrid ncini Hispania.

Muda wote walipokuwa safarini kutoka Lisbon mpaka Coimbra, Madam S hakuzungumzia lolote kuhusu nini Amata alikipata katika tafutishi zake usiku ule. Wakiwa wameketi kwa kutazamana huku pombe kali ikiteketea kati yao, ndipo mazungumzo haya ya wawili yalipoanza.



Muda wote walipokuwa safarini kutoka Lisbon mpaka Coimbra, Madam S hakuzungumzia lolote kuhusu nini Amata alikipata katika tafutishi zake usiku ule. Wakiwa wameketi kwa kutazamana huku pombe kali ikiteketea kati yao, ndipo mazungumzo haya ya wawili yalipoanza.

“Kuna lolote?” akauliza. Mtindo huu wa maswali, ulipendwa sana na mama huyu.

“Kubwa kuliko unavyofikiri. Nimekuta nyumba tupu, maskani ya buibui tu, laptopa mpoja katika chumba cha kulala…” akamjibu huku akijimiminia bilauri nyingine na kuijaza pomoni.

“Umeibeba?”

“Ya nini mimi? Nimeng’oa tu hard disc. Lakini kabla sijatoka, Dana akaja na mtu mwingine, wakaichukua ile laptop,” akamweleza.

“Dana!” Madam S akashangaa.

“Ndiyo, Dana, yaani D-A-N-A,” Amata akajibu na kwa kusisitiza akamtaji herufi moja moja ya jina hilo.

Ukimya ukajidai kati yao, wakati mhudumu wa ndege hiyo ndogo ya kifahari akiwapatia vinywaji vingine. Ilikuwa ndege ya kifahari sana, private jet yenye kasi ya hatari. Alipomaliza, akawaacha na kuondoka zake. Madam S akajikohoza baada ya kumwona Amata akiwa bize kumkodolea macho yule mwaDanada.

“Yeyote amtazamaye mwanamke na kumtamani, amekwishazini naye moyoni…” Madam S akamtania Amata kisha wote wakacheka na kugonganisha viganja vyao.

“Maneno ya kale hayo… ukiyaleta sasa basi wote tutaingia motoni,” akamwambia Madam S.

“Ok, tuyaache hayo. Tutakapokuwa Madrid tutaachana na kila mtu atasafiri kwa ndege yake. Tuonane Dar es salaam, Shamba,” akapiga funda moja na kisha kuiteremsha bilauri yake kwa madaha, “by the way, tuna kazi numu sana ya kuwaangusha hawa wawili waliobaki…”

“Nikukatishe Madam, siyo wawili, kuna wengi katika hili, lazima tuhakikishe tumeng’oa mzizi mkuu,” Amata akasema.

Kamanda Amata aliendelea kugida pombe kwa fujo. Madam S alibaki kumtazama tu pasi na kuuliza neno. Mara mlangowa mudumu ukafunguliwa, yule mwaDanada wa awali akaingia tena.

“Tumekaribia kutua, muwe tayari,” akawaambia. Amata na Madam S wakatazamana, wakashanaa kutangaziwa kienyeji namna ile. Dakika thelathini na tano baadae, walikuwa ndani ya Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Madrid au kama unavyojulikana Adolfo Suarez Madrid-Barajas Airport. Kila mtu alikuwa na hamsini zake kana kwamba hawajuani.

* * *


DAR ES SALAAM SHAMBA


Katika ofisi ya siri kabisa, iliyojengwa ndani ya jumba hilo, Madam S alikuwa mbelea ya meza yenye ukubwa wa wastani. Juu ya meza hiyo kulikuwa na kabrasha lililopambwa na jina ‘ZE SINDIKET’. Taratibu, akalifunua mpaka kurasa ya tatu ambapo palikuwa na majina manne. Akacukua kalamu yake nyekundu na kulikata jina la Vincent Mwanachia. Kisha kwenye kompyuta iliyo mbele yake, akaingiza taarifa za kifo hicho na jinsi kilivyotekelezwa. Alipojiridhishana taarifa yake, akaipakia kwenye seva kubwa inayotumika kutunza siri za serikali za usalama wa taifa kwa ujumla.

Mbele yake, sasa palikuwa na majina mengine mawili; Kibwana Mtokambali na James Msambamagoya. Hapa akili na mawazo yake viliweka nukta. Aanzie wapi? Ilikuwa ngumu kupata jibu la swali hilo. Kazi ya kujua ni wapi maficho ya Titus Mwakibinga yalipo, ilichukua miaka kama mitatu hivi kwa TSA. Kazi ngumu iliyofamnywa na Gina akisaidiana na Chiba. Alkadhalika kugundua maficho ya Vincent mwanachia, nayo ilikuwa kazi yenye utata kutokana na usaliti uliokuwa ukifanywa na watu wachache waliokuwa katika kitengo cha usalama katika Ubalozi wa Tanzania nchini Ureno.

Madam S, kichwa kikamzunguka, uso ukasawajika. Akalitazama jina la aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje, miaka ile, Kibwana Mtokambali. Alivyokuwa mtiifu kwa Rais. Alivyokuwa mchapakazi, mwenye kucheka na kila mtu. Hata Rais mwenyewe alikuwa akimtumia kama mfano kwa wengine kwa jinsi alivyokuwa akiwatendea watu wa jimbo lake. Alijenga shule, hospitali na mambo mengine mengi. Hakuna aliyejua, kumbe nyuma yake kuna mambo mengi ya siri. Kibwana Mtokambali.



* * *


1980


Mara tu baada ya kuingia kwenye duka la Kanjibhai, Waziri Kibwana alipitiliza mpaka katika kaunta ya duka hilo. Mhindi yule wala hakuumiza kichwa, alimjua Kibwana vyema, alifahamu nini anafanya. Kwa namna moja au nyingine, alikuwa msiri wake. Kanjibhai, alimtazama Kibwana jinsi alivyosawajika uso. Hakuwa na maswali, alimfunulia moja ya kabati kubwa na mzee huyo aliingia ndani yake. Mlango ukafungwa. Kabati likabaki kama kabati. Kibwana kapotelea ndani yake.

Mlango wa kabati lile, ulimfikisha Kibwana Mtokambali katika sebule ndogo nadhifu. Hakuwa peke yake, pale alikutana na vijana wawili watanashati. Prakesh na Kumeil.

“Mambo yameharibika,” akawaambia huku akivua koti la suti yake na kulitupia kando.

“Kwa hiyo tufanye mpango uliokusudiwa?” Prakesh akauliza.

“Yes! Ofcourse!” akajibu, “yaani kwa sharia za nchi yetu, natakiwa kuhukumiwa kifo. Sitaki hilo litokee kabla sijauona ukweli wa ndoto zangu…”

“Na kwa nini ufe kabla hujatimiza ndoto zako?” Kumeil akaongeza kusema.

Kumeil na Prakesh wakamchukua Kibwana na kuingia naye katika cumba kingine. Ndani ya kile chumba kulikuwa na mitambo tiba michache.

“Keti hapa!” Kumeil akamwambia Kibwana. Naye akafanya hivyo. Kazi ya kumbadilisha sura na umbo lake vikachukua nafasi ndani ya chumba kile. Kibwana hakuwa na ndevu, zikaoteshwa za bandia ndani ya dakika kumi tu. Macho yake yakafanyiwa maarifa madogo tu, yakawa na utofauti na yale ya kwanza.

“Hawataweza kukugundua,” Prakesh akamwambia.

“Kama ni hivyo si nibaki tu!” Kibwana Mtokambali, akawaambia vijana wale wakati akibadilisha mavazi yake. Muonekano wake ulikuwa tayari na utofauti ambao kwa teknolojia ya wakati ule ingewachukua muda kumundua hhasa kwa nchi zetu za Kiafrika ambazo kila kitu tupo nyuma.

“Miaka haisimami mheshimiwa,” Kumeil akamwambia.

“Kadiri dunia inavyozunguka katika mhimili wake na kubadilisha majira ya mwaka. Basiujue kuwa hata teknolojia inabadilika. Tusipokufanyia surgery ya uhakika labda utajificha kwa miaka miwilia tu. Utagundulika,” Prakesh akamwambia kibwana.

Wakati yote hayo yakiendelea, tayari Waziei Kibwana Mtokambali, alikuwa katika mavazi mengine. Suruari moja ya kijivu iliyomwagika upande wa chini, raba moja matata sana kwa kizazi hicho iliyoshonwa kwa litambaa cha Kodroy. Mara baada ya hapo, wakamchukua mpaka uwani kulikokuwa na gari moja aina ya Peugeot 504, wakaingia na kuondoka zao. Walipita pale pale nje na hakuna ambaye alimtambua. Kibwana akatoroshwa namna hiyo.

* * *


KIKAO CHA SIRI


Ndani ya chumba kidogo katika Ikulu ya Dar es salaam, kikao cha siri kilifanyika baina ya watu watatu tu; Mkuu wa Nchi, Makamu wake, Chameleone kama mwanausalama namba moja wa Rais na Mkuu wa kitengo cha Usalama wa Taifa.

“Tunahitaji kuboresha idara yetu ya Usalama wa Taifa,” Chameleone akaliambia jopo.

“Tunakusikiliza…” Rais akamwambia.

“Mpaka haya yote yanatokea, ina maana idara yetu kuna sehemu tunakosea. Kama unakumbuka katika jaribio lililopita miaka ile ya sabini, mheshimiwa ukafanya mabadiliko na kuunda kikosi maalumu cha usalama wa Rais. Lakini katika chunguzi zangu na watu wangu wa karibu,tumekaa na kuona nini cha kufanya katika kuimarisha usalama wa taifa letu…” Chameleone akazungumzakwa hisia iliyoonekana katika macho yake.

“Endelea…” Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa akadakiza.

“Mheshimiwa Rais, yatupasa kuweka mapandikizi katika idara zote za binafsi na serikali, ili tuweze kukusanya taarifa zozote za uovu dhidi ya serikali na watu wake,” akawaambia. Wote wakatikisa vichwa. Yule mkuu wa idara ya usdalama wa taifa akawa anaandika mambo kadhaa katika kijitabu chake.

“Nina maana kwamba,tupenyeze watu wetu wa UT katika hizi idara, mahospitalini, mashuleni, vyuoni wawe kama wanafunzi na wakufunzi au hata wafanya kazi wa kawaida. Lakini pia tuwawekehata katika sekta za kijamii yaani zile binafsi. Hawa wote kai yao iwe ni kutukusanyia taarifa na kutuletea na sisi tutakuwa tukizichambua na kugawanya zipi ni confidencial, secret na top secret,” akazungumza kwa umakini akiweka na misisitizo kadhaa katika hayo.

Kikao kile kilichukua takribani saa tatu. Mipango ikasukwa, ikawekwa sawa, na utekelezaji ukawa ni jambo linalofuata.

“Sitaki kusikia serikali yetu ikinyanyaswa namna hii,” Mkuu wan chi akasema huku akiiweka vyema fimbo yake juu ya meza.

* * *

Akatutoroka namna hii! Madam S akawaza. Akaachana na jina la huyo Kibwana Mtokambali. Moyoni mwake akajiapiza luwa lazima ampate kwa udi na uvumba. Kama ingekuwa ni muvi basi angeiita, ‘Two Down, Two to Go’. Lakini bahati mbaya haikuwa hivyo, tayari kabrasha lilipewa jina, Ze Sindiket.

Wakati jaribio hili likitukia, Madam S au Selina kwa jina lake, alikuwa akihudumu katika Ikulu ya Dar es salaam, kitengo cha itifaki. Mkuu wake katika kitengo hicho alikuwa James

Msambamagoya. Bonge la mtu, kaenda hewani na kupambwa kwa mwili mkubwa kama Goliath. Hakuwa muongeaji, mambo yake mengi yalikuwa ya kimya kimya tu. Selina alimheshimu kwa kile alichokuwa nacho bwana huyu. Yeye na Chameleone walikuwa nafasi za juu sana katika idara hii ya usalama wa Rais. James, aliitumia nafasi hiyo vyema, akadanganywa na kulaghaiwa na wachache wenye kupenda madaraka. Wakamtumia kama mmoja wa vyanzo vya habari. Pamoja na uintelijensia wake, akajikuta ndani ya Ze Sindiket. Akasaliti ofisi.

“James! Mienendo yako siielewi siku hizi, kuna nini?” Chameleone alimtupia swali hilo siku saba tu kabla ya jaribio lile kufanyika.

“Hapana mkuu!” alimjibu, “hali hii hunitokea tu hasa mambo yangu ya kifamilia yapokuwa yanaenda kombo”.

“Pole sana, jitahidi usiwe katika hali hiyo kwa kuwa kazi yako inakuhitaji daima kuwa makini,” akamuasa. James akajibu kwa kutikisa kichwa.

Ndani ya ofisi ya Chameleone, siku hiyo hiyo, alikutana na Selina. Binti huyu, aliyekuwa na umri sawa na bintiye, alimpenda sana. Akiwa katika kitengo cha usalama ngazi ya wilaya huko Maswa, ndipo Chameleone alipomwona. Umakini na uhodari katika kupanga mipango vilimkosha, akakosheka. Ilikuwa ziara ya kikazi ya Mkuu wa nchi wilayani hapo. Ambapo Selina akiwa katika kamati ya itifaki alionesha umakini sana katika kazi yake, mwepesi wa maamuzi na utendaji. Chameleone akavutiwa. Achana na hilo, alikuwa mrembo, uso wa duara, matiti ya wastani na tumbo lililokuwa ndani kidogo. Hipsi zake zilitengeneza mabisto ya kumvutia rijali yoyote yule.ijapokuwa yalikuwa ndani ya sketi, lakini hayakuficha mnyumbuliko wake. Akitembea, kama nguva ndani ya bahari.

“Huyu ni nani?” Chameleone alimuuliza Simbaulanga. Mkufunzi katika chuo cha mafunzo ya askari kanzu, Mbweni. Ilikuwa ni miezi saba kabla ya jaribio lile la mapinduzi.





Huyu ni nani?” Chameleone alimuuliza Simbaulanga. Mkufunzi katika chuo cha mafunzo ya askari kanzu, Mbweni. Ilikuwa ni miezi saba kabla ya jaribio lile la mapinduzi.

“Mmoja wa wahitimu wangu wenye IQ ya juu sana,” akamjibu. Chameleone akatikisa kichwa juu chini kukubaliana naye.

“Vipi? Unataka awe bi mdogo?” akamuongezea swali.

Chameleone akasikitika, akatikisa kichwa kushoto kulia, “siwezi, huyu ni sawa na binti yangu.”

“Hapa ndiyo kituo chake cha kazi?”

“No! niliagiza aletwe hapa kwa kazi maalumu tu. Ataimaliza leo hii na atarudi chuoni…” Simbaulanga akamjibu Chameleone. Mazungumzo juu ya binti huyo yakapamba moto.

Walipokuwa ofisini siku hiyo, Chameleone alimwambia Selina, “sikiliza binti… nakupa kazi ya siri, na uifanye kwa umakini”. Selina alitulia kimya akisikiliza kwa umakini.

“Nahitaji umfuatilie au umchunguze James… ila uwe makini sana asijue hili. Nataka unambie, akimaliza kazi hupendelea kwenda wapi, na nani ikiwezekana nipe hata orodha ya marafiki zake anaokutana nao mara kwa mara,” akamwambia. Selina hakuwa na hiyana katika hilo. Alilipokea na kuahidi kulifanyia kazi kwa kiwango cha hali ya juu.

Siku ambayo Mkuu wa nchi alimwita nyumbani kwake na kumpa ile taarifa ya watu hatari, jina la James halikuwapo. Lakini katika orodha hiyo alikutana na majina mawili ambayo Selina alimletea majibu kuwa ndiyo washirika wake wakubwa. Na ni mara tatu amemwona nao katika baa ya Banana huko Ukonga. Chameleone akaliweka kumbukumbuni.

Katika mshikemshike wa siku ya tukio, wakati ambapo wengi waliotumbukizwa katika jaribio lile kukamatwa. James hakuonekana. Alikwenda wapi? Hakuna anayejua. James alikuwa mlinzi namba mbili wa Rais, chini ya Chameleone, anayejua nyendo na ratiba za mkuu wake.

“Yupo. Katika mpangilio wa ratiba zake, usiku huo ataupitishia nyumbani kwake. Nafikiri eneo zuri la kutekeleza kazi hii ni nyumbani. Ikulu hakuingiliki,” James alivujisha siri wakati Sindiketi ilipokuwa imekutana kwa siri.

“Tunamuua au tunamteka?” aliuliza Vincent Mwanachia kwenye kikao hicho.

“Hatekwi. Mpango ni kumuua kabisa…” akawaambia. Mipango ikasukwa, akatafutwa mtu maalumu wa kudungua, atakayeweza kutumia risasi moja tu kuusimamisha moyo wa kiongozi huyo. Baada ya mpango ule kugundulika na kila kitu kwenda alijojo, kikao cha siri cha Sindiket kikakaliwa na uamuzi ulikuwa ni kila mmoja atafute njia yake.

James alitoka katika chumba cha mkutano akiwa mwenye mawazo mengi. Hakuwa na muda wa kupoteza. Alipoegesha Landrover lake, ndipo alipoliacha. Hatua mia moja na hamsini zikamfikisha katika nyumba moja anayoijua sana. Ya Husna. Husna, mpenziwe za muda mrefu. Siku hii alikwishamwambia atangulie Zanzibar naye angeunana huko kwa mapumziko. Hesabu zake zilikuwa kwamba siku ya kuungana na mpenziwe huyo Zanzibar, tayari anekuwa Waziri mwenye wizara nyeti katika serikali hiyo mpya. Haikuwa hivyo. Moja jumlisha moja alijikuta anapata kumi na moja.

Akaingia katika chumba cha kulala cha mwaDanada huyo. Ndani ya kabati kubwa la mbao za mninga, alivuta shubaka lililokuwa sehemu ya chini. Akalifungua na kutoa vitu kadhaa ndani yake. Baada ya kuhakikisha kila anachokitaka kipo. Akavua nguo alizovaa na kuvaa zingine. Ndevu za bandia na nywele zikatiwa mvi kiasi. Mbele ya kioo alijiona wazi jinsi alivyobadilika, mtu mzima. Kanzu ilimkaa sawasawa, balaghashia iliyotoboka upande mmoja ilikipamba kichwache.

Bila kuogopa, akatoka nadni ya nyumba hiyo na kupanda UDA, tayari kwa safari. Basi zima mazungumzo yalikuwa hayo hayo. Alisikiliza kwa makini sana ili asikie wananchi wanazungumza nini, jaribio la mapinduzi. Mara kwa mara alijikuta akipata ganzi. Basi lile, likamshusha Stesheni. Pale akatembea mpaka bandarini.kwa kuwa alikuwa akijua mpaka ratiba zote za meli, akaabiri kwenye meli ya MS Mtwara iliyokuwa tayari kuondoka kuelekea Lindi mpaka Mtwara.

Siku moja baadaye, James Msambamagoya, alikuwa katika mji wa Mtwara. Hakuthubutu kabisa kuingia mjini kwa maana alijua anaweza kukamatika. Akapita njia za panya mpaka mpakani. Akavuka na kuingia Msumbiji bila kipingamizi, akapotelea huko.

* * *

Ilikuwa ni siku ya pili tu, baada ya Madam S na Amata kufika Dar es salaam. Kazi ilikuwa bado ya moto, jukumu walilopewa, shuruti walimalize. Akafunga kabrasha lile na kulisukumia kando. Akataka kujaribu kulisahau kidogo, haiwezekani. Mlango ukagongwa, akatazama kwenye luninga yake na kumwona agongaye, akabonyeza kitufe na loki ikajiachia, ukafunguka.

“Karibu!” akamkaribisha. Kamanda Amata akaketi kitini akimtazama Madam S, “Upo sawa?” akamtupia swali.

“Ndiyo.”

“Amata, naomba uendelee kushughulika na hili swala mpaka ulifikishe mwisho. Hata kama ikiwa miaka mitano…” akamwambia na kumsogezeas lile kabrasha.

“Haina shaka, kila kitu kitakamilika, promise!” Amata akamjibu na kusimama.

“Unaenda wapi sasa?” Madam akamuuliza.

“Naelekea idara ya utambuzi, nina kazi hapo,” Amata akajibu na kuondoka zake.



HALI YA HEWA siku hii ilikuwa ya mawingu kiasi, bahari ilitulia na kuruhusu mawimbi ya wastani yajidai. Mc Tee alisimama kwenye ukingo wa baraza ndogo ya nyuma yake. Mkononi alikuwa na kitua mfano wa ubamba wa apple. Alikuwa akibofya hapa na pale huku akiongea maneno machache tu kupitia kifaa mmalumu kilichounganishwa na sikio lake.



Mkononi alikuwa na kitua mfano wa ubamba wa apple. Alikuwa akibofya hapa na pale huku akiongea maneno machache tu kupitia kifaa mmalumu kilichounganishwa na sikio lake.

Dakika chache baadae, kutoka majini, karibu kabisa na pale aliposimama, kikaibuka chombo ukubwa kama wa Volkswagen Beetle na kutulia juu yake. Upande wa juu ukafunguka, akateremka mwanaume mmoja mwenye tambo kubwa, ndevu zilizojaa kidevuni mwake zilimfanya aonekane kama gaidi Fulani.

“Karibu sana Comrade!” Mac Tee akamkaribisha mgeni wake na kumwongoza mpaka katika sebule ndogo.

“Bi Jesca vipi?” yule bwana akauliza.

“Tumtarajie dakika chache tu zijazo,” Mc Tee akajibu. Katika sebule hiyo kulikuwa na watu wawili tu yaani Mc Tee na huyo mgeni ambaye aliingia muda huo. Hakukuwa na mtu mwingine yeyote. Punde tu upande wa nje, akaibuka mpiga mbizi, akakwea ngazi mpaka kibarazani. Mc Tee akatoka kibarazani hapo na kumshuhudi mwanamke huyo katika mavazi ya kuogelea na mtungi wake mgongoni.

“Karibu sana Jessy! Big J ameshafika, ulikuwa ukisubiriwa wewe tu,” Mc Tee akamwambia yule mama.

“Asante nimekaribia,” Jesca akajibu na kuvuta hatua mpaka ndani ya sebule ile.

Ukimya ukachukua nafasi yake. Mc Tee akasimama na kuwataka wengine nao kufanya vivyo hivyo. Wakasimama kwa nukta kadhaa. Katika meza iliyo katikati yao wakawasha moto kwenye utambi mdogo uliyoloweshwa mafuta mazito ndani ya kibweta maalumu. Wakafunga mikono na kutulia kimya kwa dakika takribani tano hivi, mpaka ule moto ulipozimika wenyewe. Hii ilikuwa kama ibada kwa kila mmoja wa wanasindiket anapopoteza maisha.

“Ni wapi tunakosea?” Mc Tee akauliza.

“Nimetumia taaluma yangu, lakini nimeshindwa kujua ni wapi tumeacha mwanya,” Big J akajibu.

“Hatutakiwi kushindwa na watu hawa, tumewajaribu mara tatu kwa kutaka kumwaga damu, tumeshindwa. Tumewajaribu mara kadhaa kuwaangusha katika sanduku la kura, tumeshindwa. Sasa wanakuja, wameshaangusha ngome yetu ya Brussels na Lisbon. Tunajipanga vipi kuweka kizingiti wasifike upande huu?” Mc Tee akaeleza na kuuliza. Ukimya ukataradadi kati ya watatu hawa.

“Mi nafikiri twende upande wa pili,” Big J akasema, “tuingize vijana wetu mjini ili wakatafiti kujua wapi tunakosea…”

Mc Tee akatikisa kichwa kukubali. Jesca akabaki kimya kabisa, hakusema lolote.

“Jambo la kufanya, kwanza ni kujua nani kakabidhiwa kabrasha huko TNS?” Mc Tee akasema.

“Tuwe makini sana, tusipoangalia, tutatafuta mtu na kusahau kazi yetu, wafadhili watatushangaa,” Jesca akatamka kwa mara ya kwanza.

“Habari mbaya ambayo hainifurahishi ni kuwa ile laptop haina diski ndani…” “Eeen! Ina maana imeibwa?” Bi J akadakiza swali.

“Ndiyo, yaani kuna mtu aliiwahi laptop akachomoa diski yake, au yeye mwenyewe Mwanachia? Sijui… kitendawili,” Mc Tee akasema.

Ukimya ukajidai kati yao, jambo hili liliwafanya wote wawe kimya. Big J akatahayari. Akapatwa na kigagaziko, mwisho hakuwa na budi kufungua kinywa, “ina maana hata hapa alituwahi?”

“Sijui kama alituwahi au imekuwaje,” Mc Tee akajibu, “cha muhimu hapa ni kufanya utafiti wa kumtambua aliyeshika hiyo laptop baada ya Mwanachia,”akaongeza wazo.

“Wazo zuri na makini, tuwasiliane na Zelda, mstaafu wa MOSSAD anaweza kutusaidia. Yule bwana ameanzisha kitengo chake binafsi cha uchambuzi,” Big J akatoa wazo. Hakuna aliyepingana nalo kwani wote waliujua uwezo wa Big J katika mambo ya Intelijensia. Daima walimtegemea kwa mipango kama au inayofanana na hii.

“Sasa sikia Big J… hapa tunachotaka sisi ni kumtambua huyo mtu. Waelekeze jamaa zako watuletee alama za vidole zote zitakazopatikana,” Jesca akatoa maelekezo.

Kikao hiki cha kwanza kufanyika bila uwepo wa Mwanachia na Mwakibinga kilikuwa kizito sana. Moja ya jambo jingine lililojadiliwa ni kuhusu kuongeza nguvu katia sindiket yao.

“Swala la kuongeza watu kuziba mapengo hayo, soliungi mkono. Kwanza itakuwa ni kama kujitokeza hadharani na kumwanikia kifua adui yako,” Big J aliliambia jopo. “Mi nafikiri tubaki kwa idadi yetu kama tops, halafu kazi yetu itakuwa ni kununua vijana na kuwapa kazi ya kufanya”. W.azo likakubalika na kupitishwa haraka.

“Lazima tutimize azma yetu. Kama ni kupindua serikali basi lazima tufanye hivyo kwa hali yoyote,” Mc Tee akawaambia wenzake, “lakini nafikiri yatupasa kutengeneza mamluki ndani yao ili tupate kujua mipango yote ya ndani dhidi ya tufanyayo,” akamalizia kusema.

“Wakati mwingine, mamluki si watu wa kuamini sana. Sisi twaweza kumpa pesa akawa mamluki, sawa, lakini nyuma yake akawa fukufuku, kwa sababu anaweza kuplay kama D.A… Sote tunajua kilichotupata mwaka 1989 kutoka kwa kijana tuliyemwamini…”

“… Dastan Kihwelo!” Mc Tee akamkata kauli Big J, kisha akamalizi na sonyo kali.

“Dastan, tulimwamini sana, ukizingatia ni kijana ambaye nilimjua ndani nje. Lakini tangu mwaka jana baada ya kifo cha Mwakibinga, naihisi athari ya kazi yake kinyume na sisi.je si mono wake katika kifo cha Mwanachia?” Big J akasema.

“Naunga mkono usemalo, alimuua Bambros. Na Bambros ndiye alikuwa na kabrasha za Mwakibinga na Mwanachia mara baada ya kikao chetu cha Sindiket pale Bagamoyo… shenzi kabisa yule!” Bi Jesca aliongea kwa uchungu.

“Na ataendelea kuhifadhi siri zetu mpaka Yesu arudi, shubamit!” Mc Tee akang’aka.

* * *


Bagamoyo 1989, Julai


Mara baada ya kikao kizito kilichokaa katika Hoteli ya Bagamoyo Sun, Babmbros alitere,mka ngazi haraka haraka kuliekea gari lake alilokuwa ameliegesha chini. Hakutaka kuongea na mtu kwa kuwa alijua wazi kuwa ni nini ambacho amekibeba mikononi mwake. Makabrasha. Makabrasha yaliyohifadhi siri nzito za sindiketi hatari kabisa kwa usalama wa nchi.

Kikao hiki kiliwakutanisha watu sita tu, watano waliokuwa upande wa wasikilizaji na mwingine mmoja aliyekuwa upande wa pili, akiwa anaonekana miguu tu na kusikika sauti. “Mwaka 1990, si mwaka wetu, hivyo tuache kila kitu kitawale kadiri ya ilivyopangwa.

mipango yetu tuendelee kuiweka sawa, na kuanzia mwaka 1995 na kuendelea basi iytakuwa ni utekelezaji tu mpaka tufikie azma yetu. Misaada yote mtapata, nguvu yoyote mnayotaka tutawapatia…”

Hili lilikuwa agizo kuu ambalo mtu huyo asiyeonekana alilitoa wakati akifunga kikao kile. Alirithi ufadhili wa babu kwa baba, akaamini naye akishindwa atamrithisha mwanawe.

Bambros, raia wa Ugiriki aliyechanganya damu na Wahehe wa huko Kidamali Iringa, aliketi katika gari lake tayari kwa safari ya Dar es salaam. Aliaminiwa akaaminika. Alikuwa mtunza siri hodari, hata umng’oe macho, kamwe hasingediriki kukwambia kitu.

“Embassy Hotel, bila kusimama mahali…” akamwambia dereva. Dereva wa gari hilo ambalo siku zote lilimbeba Bambros kwenye harakati zake, akajibu kwa kutikisa kichwa. Akawasha injini, ikaitika. Akatumbukiza gia ya kwanza, ikatii. Lile gari likayaacha maegesho taratibu na kuikamata barabara ya kuelekea Dar es salaam kupitia Bunju mpaka Boko. Saa mbili tu, dereva alizitumia kumfikisha hotelini hapo.

“Utanifuata saa nane usiku, utanikuta hapa hapa!” akamwambia huku akiteremka. Yule dereva akaitika kwa kichwa kama mwanzo. Bambros akatilia mashaka tabia hiyo mpya ya dereva wake, lakini hakuifatilia. Akavuta hatua na mkoba wake mkononi, akamezwa ndani ya hoteli hiyo ya kimataifa. Dereva wa gari lililomleta Bambros alirudiwa na fahamu akiwa ndani ya buti la gari mara baada ya kusimama pale Hoteli ya Embassy. Hata alipojitahidi kugonga hakuna aliyemsikia. Nyuma ya usukani wa gari lile, Dastan aliendelea kumtazama Bambros akipotelea hotelini humo.

“Nitakutembelea baadae!” akajisemea kwa sauti ndogo kisha akaliondoa lile gari mpaka kwenye mzunguko wa saa akaliegesha kandokando ya duka la Magereza. Akateremka mara tu baada ya kufyatua kifungulio cha buti hilo na yeye kutoweka. Hatua kama mia mbili hivi baada ya kuuacha Mtaa wa India, akakunja na kuchukua Barabara ya Morogoro. Mbele kidogo kuliegeshwa gari dogo aina ya Toyota Corona. Akaingia na kuketi kwa utulivu. Dakika kama mbili hivi baadae, kioo cha upande wa pili kikagongwa, akafyatua mlango na kuruhusu mtu wan je aingie ndani.

“Umefanikiwa Dastan?” yule bwana akamuuliza.

“Hatua ya kwanza tayari, kazi iliyobaki ni kwenda kuzibeba tu,” Dastan akajibu kwa utulivu, mkono wake ukavuta droo na kuchukua Big G akaimenya na kuitia kinywani.

“Saa ngapi?” yule bwana akauliza.

“Kama saa sita hivi maana saa nane anatoka,” Dastan akajibu.

“Ok, nafasi nzuri, nafikiri subiri anapotoka ndiyo ukachukue…”

“Hapana! Kama unataka kupata unachotaka, pambania kufa na kupona. Ukisubiri wepesi , utapata usichotaka,” akamgeukia yule jamaa, “Namjua Bambros, anajua kutunza na kuficha siri, nikienda muda huo unaosema, nitakuta magazeti ya Mzalendo na Mfanyakazi tu,” akarudisha macho mbele.

“Ok fanya unaloweza, cha muhimu ni kupata tunachotaka,” yule bwana akamwambia Dastan. Mbele ya gari lile, kulikuwa na mwanamke aliyekuwa akija taratibu kwa mwendo wa kudengua. Mavazi yake yalionesha wazi kuwa ni dada poa. Dastan akapiga honi mara tatu.

“Aaaa Dastan vipi? Unajua mwakaniunaoa wewe, sasa hawa malaya wa nini?”yule jamaa akamlaumu Dastan.

“Tupo kwenye biashara kaka, ye anauza, mi nanunua!” Dastan akajibu wakati yule mwaDanada akifungua mlango na kuingia.

“Karibu Aziza!” Dastan akamkaribisha huku akifungua droo ya kwenye gari. Akatoa kitu kama mkebe na kumpatia, “zawadi yako niliyokuahidi ni hii,” akamkabidhi. Aziza akapokea na kuitia mkobani.

“Leo nataka uniue kitandani kwa mapenzi makali, nimejiweka tayari kwa ajili yako,” Aziza akamwambia Dastan huku akifungua mlango na kushuka.

“Bila shaka, niko ngangari… risasi tatu za kichwa zitakuacha hoi kitandani,”

“Mmmm uwe na shabaha tu katoto…” akaubamiza mlango na kupotelea kwenye mataa ya mjini.

“Vijana mna matatizo sana!” yule bwana akasema, “ina maana mpenzi wako hakutoshi mpaka unakuja kubeba vya barabarani?” akamuuliza.

“Haniridhishi hata kidogo. Ngoja nikamchakaze Aziza!” akamwambia yule jamaa na kuagana naye.

* * *

Aziza aliwasili Hoteli ya Embassy usiku huo. Ujio wake katika hoteli hii ilikuwa ni miadi yake na bwana Bambros au Mtupesa kama alivyopenda kumwita. Alipofika wala hakuuliza, akakwea ngazi taratibu kwenda ghorofani huku akivaa heleni zake alizopewa na Dastan kule garini zikiwa ndani ya mkebe. Dakika chache zilizofuata, alikua ndani ya chumba cha Bambros, akapokelewa na mabusu mazito yasiyo na idadi.

Bambros alipenda sana wanawake, hakujali ni kiasi gani cha pesa angetumia kwa ajili hiyo. Akiwa katika jiji la Dar es salaam, jambo lakwanza alilolifanya ni kutafuta mwanamke wa kumburudisha kila usiku anaokuwa kitandani. Akawapata kadha wa kadha. Dastan alipoujua udhaifu huo akapanga kuutumia vyema katika misheni yake mara baada ya kujiuna na kundi hili hatari. Kundi hili liliamini kuwa Dastan atakuwa mtu safi kwa kuwa atawaletea habari nyingi za siri za serikali juu yao na mpango ya kiutawala kwa kuwa alikuwa ni mwanafamilia wa Usalama wa Taifa. Wakati huo huo, familia ya Usalama wa Taifa ilimuuza kwenye kundi hilo ikitegemea kupata siri za mipango na mikakati yao aghalabu kujua wasakwa wao wako wapi, akina Mtokambali na wengine.

Kifaa cha masikioni alichokivaa Dastan, kilimwezesha kusikia mazungumzo ya Aziza na Bambros. Hata heka heka za kutaka kutupana kitandani alizisikia vyema.

Muda umefika! Akawaza akiwa anavaa gloves mikononi mwake. Akaliacha gari lake mtaa wa nyuma wa hoteli hiyo. Kupitia upande huo huo, akakwea ngazi za dharula mpaka skafu aliyoihitaji. “Nitalalaje na wewe wakati hujanilipa?” Sauti ya Aziza iliyatekenya masikio ya Dastan.

“Oh Sweet heart, kila kitu utapata! Kama shida ni pesa tu jichukulie kwenye briefcase hiyo hapo juu,” sauti ya Bambros ilisikika ikimjibu.

Dastan akafungua mlango na kuingia kwenye korido ndefu ya ghorofa hiyo. Viatu vyake vya mpira havikumfanya asikike. Akatembea tarataibu kukifuata chumba alichokikusudia. Alipoufikia mlango akatulia. Kupitia kile kifaa alianza kusikia miguno ya mahaba ya wawili hao ikishika hatamu.

“Mmmm uwe na shabaha tu katoto…” maneno ya Aziza yalimrudia kichwani, akauma meno.

“Darling, fika haraka, darling jamani… fi-fika!” Aziza aliongea kama mwendawazimu akiwa kitandani na Bambros. Kijana huyo alijua mwanamke aliyenaye usiku huo kanogewa na manjonjo yake. Nje tu ya mlango wa kile chumba, Dastani alikuwa keshaikamata sawia bastola yake. Moyo ulimwenda mbiyo, akapumua kwa nguvu. Aliupata vyema ujumbe wa Aziza kuwa afike wakati huo.


ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

BLOG