Search This Blog

Saturday, February 26, 2022

SIHITAJI KURUDI NILIKOTOKA - 4

   

Simulizi : Sihitaji Kurudi Nilikotoka 

Sehemu Ya Nne (4)



" Yuko room.

" Pliz nakuomba nionane nae naitaji kumuomba msamaha.

" Wewe weweee!, wewe deniss wewe!, kipigo ulichopewa jana hujaridhika unataka chengine ee!, ninachokuomba mpenzi wangu kaa mbali na yule mwanadada atakunyoosha, yule haombeki msamaha na kuna mambo yamemharibu kisaikologia ndo maana yuko vile, kaa nae mbali kabisaaa kwa usalama wako, ukimuona kimbia na usije kutaka kumfanyia mchezo mchafu wowote, jana beach huko kawakung'uta wanaume hao!. Alisema maryam kwa hisia akaonesha vidole vinne.

" Wanne. Deniss aliekuwa kimya kusikiliza kile anachopewa, alimalizia kwa kusema wanne.

" Enheeeee wanne babaangu kama wamesimama kawatembezea kichapo.

" Dah!, sikiliza maryam mimi siko kwa nia mbaya naitaji kumuomba msamaha yaishe tuwe kiamani, mambo ya uadui hayafai alafu sote tuko chuo inakuwa sii vizuri, naitaji kumuomba msamaha tafadhali mwambie. Alisema deniss huku tumbo likiwa joto kwa habari aliyopewa.

" Tatizo lako deniss uliitaji kujifanya bangi ukidhani amelegea, kumbe mwenzako bangi zaid yako sasa shauri yako, baada ya kupigwa ndo unataka amani, kama wewe ungempiga akaja kukuomba amani na ulivyokiburi ungemkubalia au ndo ungezidi kumtukana?.

" Usiseme hivyo maryam najua wewe ndo rafiki yake na ndo wa kunisaidia mimi pliz pliz nakuomba.

" mimi huo ugomvi bhana siuingilii, siuingilii kabisaa maana nguvu zangu zenyewe zinaitaji nguvu za ziada ili ziwepo, aya nimkoroge anigeukie mie anipe kipondo na mkono wake ulivyo haram kupiga vile unataka nife?, nashukuru tu kwa kuwa rafiki yake na kunikubalia urafiki. Kuhusu hilo jambo lako msubiri akiingia class umuombe. Alisema maryam. Muda huo huo lucky mwenyewe alikuwa anaingia eneo hilo, walikuwa karibu na kikorido na yeye alitokea kwenye kona hivyo walikuja kumuona akiwa tayari amewafikia, Deniss mapigo ya moyo yalianza kwenda mbio akahisi kiyama kimemfikia alipomuona, kidume alitetemeshwa vibaya na mtoto wa kike ambae hakuonesha dalili zozote za kuwa mshari.

" Huyo hapo mwambie yale ulotaka kunituma. Alisema maryam.

" Mambo?. Alisema Lucky kumsalimia maryam.

" Poa ndo unaingia pindi?.

" Yah ndo naingia!, naona uko na hanisi la kiume.

" Mh!, lucky taratibu basi naomba upite uende class pliz my lovely friend.

" Nishikie mkoba wangu. Alisema lucky.

" Unataka ufanye nini?.

" Wee nishikie mkoba.

" Lucky usifanye hivyo bhana. Maryam alianza kulia lia akijua kabisa anataka ashikiwe mkoba ili alianzishe.

" Kama hutaki sema. Alisema kwa kufoce maryam ikabidi aushike, Deniss kukimbia alihisi ni aibu kubwa ikabidi abakie tu kibishi, miguu ilikuwa inatetemeka moyo wake ukawa hauna amani, hata kuongea nisamehe lucky alishindwa.

" Wewe ndo hodari wa kuwatukana watoto wa kike hapa chuoni sio?. Alisema lucky.. Mimi nawategemea mabwana wanikaze ndo nipate ada ya chuo room na kula si ndio?.

" Hapana. Alisema deniss kwa kutetemeka.

" Usiseme hapana kwa sauti ya kulegea hivyo wakati umeambiwa na dem ulietaka kumdhalilisha si kidume mwenzako, Nataka nikuoneshe huko kuwategemea kwangu mabwana kunavyonipa nguvu za kumshughulikia mtu, ntapambana na wewe kila ntapokuona kwa sababu tusi lako moyoni mwangu haliwezi kutoka, nlikukalia kimya mwaka mzima tokea naingia chuo ukiwa unanifata fata na kukuambia kiustarabu kuwa sitaki ukaniona fala, sikuwahi kukujibu vibaya kukutukana wala kukusonya, ila wewe ukajiona mdomo mrefu kwa ufahari wako ukaona umtukane lucky, tupigane ili ionekane kati yangu na wewe nani anawategemea mabwana hapa chuoni. Alisema lucky, kila alipokuwa akiongea munkari kichwani ulikuwa unapanda, alimkunja deniss nguo yake kifuani na kumuitaji wapigane ataeshindwa ndo atakuwa anategemea mabwana, maneno hayo yaliyozungumzwa na kijana huyo yalimuuma sana lucky kama mtu anaejielewa anapotukaniwa wazazi wake au mama yake, kwa hilo tusi la yeye kuwategemea mabwana chuoni alihisi ametukanwa tusi kubwa zaid ya mtu kumtukania mtu mama yake...


" Lucky naomba tusameheane, nakubali nlikosa ubinadam nisamehe yaishe. Alisema deniss kijasho kikiwa kinammiminika usoni hadi kwenye uti wa mgongo, sura ya lucky ilishachafuka uzuri wake wote uliisha.

" Kwa kuwa yamekufika shingoni ndo unaitaji msamaha, vipi siku uliyotaka kuniaibisha ningekuwa dhaifu si ungenichafua?. Usitake kumuonea mnyonge hali ya kuwa ukionewa wewe unaumia. Alisema lucky kwa sauti ya upole kisha akaanza kumshushia makofi ya adabu, yalikuwa yakuchanganya mwisho alimkamua kichwa bila kuhofia kuharibika kwa nywele zake alizokuwa ameziweka vizuri kwa mtindo wa kirihanna, Maryam machozi yalimtoka akaanza kulia akipiga piga miguu chini, kuamlia alikuwa hawezi ikabidi apige kelele ili watu wasogee, bahati nzuri au mbaya wakina tunu nao ndo walikuwa wanatokeza eneo hilo.


Walishangaa sana kumuona Lucky akiwa amemng'ang'ania mwanaume ambae walikuwa wanamjua vizuri kwa kujisifu kwake pamoja na kujidai kwa pesa alizonazo, Amina alishagawa penzi kwa kijana huyo tunu nae alikuwa kwenye harakati, hawakutaka kuamini hata kidogo kama ni lucky huyo huyo wanaemjua wao mkimya muda wote chumbani ndo anagawa dozi ya vurumai, watu walizidi kusogea taratibu mpaka maprofesa, walifanikiwa kuamulia huo ugomvi ila tayari deniss alikuwa ametoka manundu usoni, jicho la kushoto lilikamuliwa ngumi nzuri tu likawa limevimba kama ameng'atwa na nyuki, alikuwa hoi zaid ya siku ya kwanza.

" Ntakunyoosha mpaka ukihame hiki chuo mjinga wewe, ulilolitaka limekuwa na kama una hamu ya kutiwa vidole makalioni panakuwasha nambie ntafanya kazi hiyo na sii kunitukana, unayajua maisha yangu yalivyo?. Au ushoga ulionao huo wa kujipodoa wanaume wenzako wakutamani wakupige mizinga unadhani na wenzako wanao!?. Alimtusi matusi ya nguoni ya kumdhalilisha ambayo mengine ngumu kuyaeleza mbele ya pablic ya watu, wanafunzi waliokuwepo walishangaa sana uwezo wa lucky kuongea maneno mazito ya aibu wakati walimzoea kuwa mkimya, wengine walijisemea mioyoni mwao kweli muogope mtu mkimya akiamua anakuwa balaa kuliko muongeaji..

" Binti kwa nini unafanya upuuzi huu hujui kama ni utovu wa nidhamu na unaweza kuchukuliwa hatua za kisheria?. Aliuliza moja ya walimu wakubwa aliekuwa anaeshimika sana na wanafunzi, ndo alikuwa anaingia ofisini kabla ya kufika akakutakana na vurumai hilo.


" Haya ni maisha yangu binafsi, kabla ya kuchukuliwa hatua za kisheria itabidi wanaotaka kunichukulia hatua wajipange, kwa nini yeye isiwe kwa mwengine?. Kuna mtu yoyote nliwahi kumtukana au kumtolea maneno machafu why yeye, Profesa hamad nakueshim sana ila nadiriki kutamka mbele yako, Ama zake ama zangu, aondolewe yeye hapa chuoni au mimi, laa sivyo ntakula nae sahani moja kila ntapoonana nae hiyo ndo kazi, anayajua maisha yangu hadi anambie mimi nawategemea mabwana chuoni kusoma?. Nliwahi kumuomba hata shiling moja baada ya kupungukiwa, mbele ya pablic ya watu anaitaji kuniondolea heshima yangu nliyonayo chuoni nimfanyaje, mara ngapi nachukua tuzo za nidhamu ina maana gani, sina ina maana mwanafunzi mtiifu msafi na asiekuwa na tabia mbovu?, why anichokonoe?. I swea my professa mbele yako naapa popote ntapomuona Denis lazima nimtembezee kipigo, kwa kuwa nguvu ninazo uwezo ninao, atajua kuwa kuna wanawake vichaa walivuta bangi kabla ya kuzaliwa kwao sii wanaume tu.. alisema lucky kwa sauti ya kupanda na kushuka huku machozi yakimtoka kutokana na hasira alizokuwa nazo, hakujali maneno hayo anamuambia nani mbele ya umati wa watu ambao ulishakuwepo, Amina na tunu walikuwa katika mshangao mkubwa wa kujiuliza huyu ndo lucky ambae wanaishi nae chumbani kwao siku zote au sie?.




" Ni nani rafiki wa huyu binti.? Aliuliza profesa alietambulika kwa jina la Hamad.

" Its me profesa. Alisema maryam.

" Mpeleke room akapumzike baada ya masaa mawili naomba umlete ofisini kwangu.

" Okey.

" Mpelekeni huyu kijana akapatiwe matibabu. Kisha aligeuka upande wa deniss akawaitaji watu wampeleke kwenye vyumba vya matibabu akatibiwe..


Maryam Alimchukua lucky akatoka nae eneo hilo, kila mmoja alikuwa haamini kilichotokea, wapo baadhi ya waliokuwepo katika tukio la mwanzo na kushuhudia hilo pia, Lucky alikuwa gumzo chuoni kwa karibia wanafunzi wote. Deniss alifanyiwa matibabu wakamuweka mabandeji usoni jichoni na kumfanyia huduma nyingine sehemu mbali mbali za mwili wake, huku maryam aliingia na lucky chumbani akafunga mlango, alimkalisha kitandani kisha nae kukaa pembeni, alimwangalia bila kummaliza akamuita..

" Lucky!.

Lucky aligeuka akamwangalia maryam bila kuitikia.

" Kwa nini unakuwa hivyo mpenzi wangu ee!, nionee mimi huruma basi mimi mbona nakuonea huruma lakini?. Alisema machozi yakimtoka. Em fikiria kila mmoja chuoni anakuchukuliaje sasa hivi, baada ya masaa mawili profesa hamad amesema twende ofisini kwake unajua kitu gani anakuitia?. Kama ni adhabu je anaitaji kukupatia. Aliendelea kusema kwa hisia.

" Niache kama nlivyo maryam, ntaishi nnavyopenda na sii wanavyopenda, hakuna anaejua matatizo yangu nliyonayo, hata ikitokea nkafukuzwa fresh tu hamna tabu, kusoma ntasoma hata mitaani lakini siwezi kuona nakosewa adabu na mpumbavu mmoja.

" Usiongee kwa utashi wa mdomo wako Lucky fikiria kwanza, kwa hiyo uko tayari kuniacha mimi hapa chuo urafiki wetu ufe kisa mambo hayo?.

" Akili zangu huwa ni mbili tu kichwani siku zote, nna akili ya kumueshim mama yangu, na akili ya kuwaza jambo lililopo sii linalokuja wala lililopita.

" Fine!, Okey Lucky, but remember i love you na nimekuzoea now siku mbili hizi, nna urafiki wa dhati kwako na siko tayari kuupoteza kwa kuona mwelekeo wako, nna imani ipo siku moja yatakwisha, siko okey ngoja niingie bafuni kujimwagia maji then twende ofisini kwa ticha au vipi?..

" Haina haja!, akili yangu inaniambia nitoke tu chuoni kwenyewe, nahisi maisha ya chuo yatanishinda so bora niachane na masomo niende kuishi maisha yangu ya kitaani. Alisema lucky.

" Eh!, kwani una nini lakini jamani lucky mbona hivyo?.

" Nakujoke ntabaki. Alisema lucky kumpoza maryam baada ya kuona maneno ya kuwa anataka atoke chuoni kwenyewe yamemuuma, lakini kichwani kwake kweli alishakuwa na mawazo ya kutoka chuoni kwani alihisi hakuna atachokifanya kikafanyika ikiwa akili zake zinazidi kuchanganywa kiasi hicho.


Waliongea maryam akaingia bafuni kujimwagia maji, lucky nae alivua nguo za class akavaa khanga nzito nakuingia bafuni baada ya maryam kutoka, walipomaliza wote waliongozana kuelekea kwenye ofisi ya profesa hamad kwenda kumsikiliza anasemaje.

" Lucky. Walipofika na kukaa kwenye viti vilivyokuwa mbele ya meza yake, walisalimiana baada ya salam profesa akamuita lucky.

" Naam.

" Akili yako iko sawa?.

" Yah iko sawa.

" Huna kitu chochote kinachokusumbua?.

" Yah sina.

" Why unafanya vitu vinavyopelekea kuondoa nidhamu yako uliyonayo kwa muda mrefu sasa hapa chuoni.?

" Nisamehe profesa ila sitoweza kukueleza chochote, zaid ya yote ntaomba msamaha lakini kujielezea kiukweli siwezi.

" Ok, nimetoka kukutetea katika uongozi wa juu, na kutokana na busara yangu nliyonayo nimeeleweka na umesameheka, nakuchukulia kama binti yangu nyumbani hasa kutokana na tabia nzuri unazozionesha, na mtoto akikosea kwa kawaida mkanye sii kumfukuza nyumbani, achana na watu piga kitabu, usimwangalie mtu anaitaji uishije, bali jiangalie mwenyewe unaishije ili uweze kufika mbali, mafanikio yako yako mikononi mwako japo kuna vizuizi vya watu wengi, mgomvi aliezoea kufanya ugomvi kumkorofisha mstaarabu ndo kazi yake, kuna watu wameumbwa kuharibu maisha ya watu na hawafurahi kuona mtu anaishi vile anavyotaka, wanapenda kuona anaishi vile wanavyotaka, wao wanataka wamuone hana furaha, maendeleo yake yanafeli, usiwaangalie hao wapite kushoto ili yako yaende. Sehemu ya kuingizia funguo katika kitasa cha mlango wako imechoka, badilisha kitasa au eneo la funguo ili wezi wasije kuiba mali zako okey!. Penye mafanikio lazima viwepo vikwazo, usizikatishe ndoto zako kwa sababu ya upumbavu wa mtu mmoja. Alisema profesa hamad akiwa anazunguka taratibu katika kiti chake kisha kumpiga fumbo dogo, ambalo haraka walijua maana yake halikuwa gumu sana kuleta maana.

" Okey asante kwa ushauri wako, ntaufanyia kazi na nisamehe sana.. alisema lucky.

Maneno aliyoyaongea bwana mkubwa yalimuingia vizuri kichwani, japo alikuwa na akili nusu lakini alipoambiwa kitu kizuri akili yake ilikishika, alimuelewa mr hamad na akawa tayari kuyafanyia kazi maneno aliyoambiwa, maryam nae alifurahi mno moyoni kwa maneno ya mr hamad, yalikuwa maneno mafupi lakini ya kuukonga moyo, alijua kweli huyo ni prifesa wa saikology hakuitwa profesa ili mradi profesa, aliamini lucky kwa maneno aliyoambiwa na jinsi yalivyoonesha kumuingia lazima yatasaidia kwa mara moja au nyingine, hakukuwa na lengine la ziada walitoka wakarudi room.


Walifika wakakutana na wakina amina tayari wakiwa wametoka class, maryam hakukaa alimwambia lucky anatoka anaenda nyumbani kwao kurudisha gari, lucky alimpa tano ya kishkaji maryam akaondoka zake kwenda mbez ya samaki, nia yake ilikuwa kwenda kumhoji mama yake juu ya mr edwad na sii kurudisha gari kama alivyomwambia lucky, alitaka kufatilia kwa gharama yoyote ili aujue undani wa lucky japo ilikuwa hatari kwake endapo lucky mwenyewe angejua.....


Amina na tunu mchana walitoka chumbani kwenda lunch.

" Rafiki yangu unaweza kuishi na mchawi usimjue hadi siku Mungu atapoamua kumkuonesha. Alisema Amina wakiwa wanashuka chini.

" Kwa nini?.

" Hivi lucky ulivyokuwa unamuona kalegea legea vile ulidhania anaweza kupigana na mtu kama deniss?.

" Hahahaaaaaaa!, mbona unanchekesha wewe?, Nlishasahau hasa tukio lenyewe, kwanza chanzo kilikuwa nini hadi kumbalaguza vile?.

" Maryam ndo wa kumuuliza swali hilo.

" na kweli atakuwa anajua, si unakumbuka maneno yake aliposema mkienda chini mtajua kama ni mshamba au sii mshamba?.

" Aaaahaaaaaaaaaa okey picha inanijia, inaonesha hili varangati ni la toka jana, ujue jana deniss nlionana nae jioni hivi, usoni kavimba vimba, mara anachechemea nkajiuliza vipi?. Alafu nkimsemesha mara anaogopa kujibu kuuuumbeeeee!!.

" Maryam akirudi atupe A to Z.

" unadhani atasema yule?.

" Kwa nini asiseme?. Namchamba kweli akileta mashauzi.

" Deniss nimemtoa hadhi kupigwa na mwanamke.

" Yani wee acha tu na atahama hiki chuo.

" Mwenyewe hapa nshaogopa kukaa kwenye hicho chumba siku anatuchenjia anatunyuka, nguvu zenyewe zilivyo mbili hivi!.

" Hhhhhm amnyuke nani?. Labda akunyuke wewe sio mimi namfungia mtaa chuo anakihama bila kutaka manina zake, anipige mie!, loh.. alisema Tunu.

" Utampiga na uembaba huo?. Mwili nyumba ule.

" Nataka uwe shamba nyumba ndogo lakini hanipigi, akinishinda nguvu mawe na meno haviuzwi..


Amina aliangua kicheko kwa alichokiongea rafiki yake, Walifika hotel wakaagiza chakula, waliendelea na story topic ikiwa ni kumuongelea lucky, jina lucky lilikuwa kwenye vinywa vya watu wengi sana chuoni, alikuwa maarufu kutokana na ukimya wake lakini sasa akawa maarufu kwa alichokifanya..


Saa nane maryam alifika mbez beach kwao akafunguliwa geti na kuingia ndani, alipaki gari akakutana na mdogo wake wakasalimiana, alikuwa na vijizawad akampatia wakaenda wote hadi seblen alikokutana na mama yake, alimsalimia akakaa chini wakafungua ukurasa wa maongezi.

" Jumaa tatu leo ulikuwa na kipindi asubuhi?. Aliuliza mama yake aliejulikana kwa jina la Ashura.

" yes!, tumemaliza mapema mno nkaona nirejee nyumbani vipi baba alipokuja hajaulizia gari?.

" Gari ni yako ataiuliziaje?.

" Weee hachelewi yule mzee, mwanafunzi yule ashaanza mambo ya starehe nimemnunulia ili ije imsaidie badae anaitumia sasa hivi mpumbavu yule ngoja aje!. Alisema akimuact baba yake anavyokuwa anaongea.

" Kwa hiyo baba yako ashakuwa mzee. Aliuliza ashura.

" Dingi eti yule uoni uso ushaanza kuisha, scrab tu ndo inamsaidia laa sivyo angekuwa kama nyani.

" Shauri yako kitinda mimba yupo hapa unamjua kwa kufijisha taarifa.. hajasema kitu aliulizia tu mbona gari moja haionekani nkasema kachukua mwenye nayo..

" Aje afikishe aone kama sijamnyuka makwenzi.

" Mama yako nae je ashakuwa kizee ee!.

" Uzuri wote huo mamaangu, wee bado mbichi sana baba akikuacha leo ukaingia mtaani lazima uwapelekeshe, jicho jicho mdomo wa lips chezea!. Alisema akiachia tabasam lililomfanya mama acheke, walikuwa kama mtu na shost yake, kwa jinsi walivyokuwa wanaongea angeingia mtu akaambiwa ni mtu na mama yake isingekuwa rahisi kuamini.. Tuachane na hayo, nimekuja hapa na kitu kimoja mamaangu nataka unisaidie. Alisema baada ya kumaliza kucheka.

" Kitu gani?. Aliuliza ashura akikaa vizuri kwenye sofa kumsikiliza mwanae.

" Kuhusu mzee edwad uliemtaja jana nlipokuja hapa na rafiki yangu Lucky..




" Mh!, wee mtoto ushaanza mabalaa yako ee!. Aliuliza ashura.

" Mabalaa gani mama?.

" Sasa unamuulizia mzee wa watu ili iwaje?.

" Dah, kwa hiyo mama una maanisha namuuliza ili awe mwanaume wangu?.

" Sasa wa nini?.

" Mama uliza kwanza kabla hujaisi vibaya.

" Wa nini?. Hamchelewi watoto wa vyuo mara nlipokuambia ana maduka kariakoo akili yako hoi, na yule mzee sii mtu mzuri labda kama kaacha sasa hivi. Alisema ashura na kumuacha mwanae njia panda, alijiuliza sii mtu mzuri kivipi, kitu kilichomchanganya akilini mwake.

" Mamaangu hujanilea hivyo, kama ndivyo ulivyonifundisha haya. Alisema maryam baada ya kuwaza vitu kichwani mwake kuhusu maneno aliyoyaongea mama yake.

" Haya nambie wa nini?. Aliuliza ashura.

" Yule rafiki yangu nliekuja nae kuna matatizo anayo. Tokea aingie chuo hatumjui baba yake mama yake wala ndugu yake yoyote, ukimuuliza kuhusu baba anaweza kukupiga ngumi, na inaonekana ametokea sehemu moja ya maisha flan mazuri ila magumu yaliyomharibu kisaikologia, naomba unielekeze kwa huyo mzee kwa sababu ulipomsema mbele yake alishtuka akaonekana kubadilika.

" Sawa, yule mzee mimi nlimfahamu mwaka juzi, ni mtu maarufu sana africa mashariki kutokana na kazi anayoifanya, ila anaonekana kuwa mzee ambae hajatulia kiukweli, mkewe ni ndugu wa mama shakira hapo jirani nyumba ya tatu.

" Mama shakira yule mbunge na mwanasheria wa chama cha chadema?.

" Huyo huyo, nlikuwa karibu nae sana siku za nyuma kabla hajawa bize, kila siku lazima alinipatia malalamiko ya ndugu yake huyo kuhusu mmewe ili tusaidiane kumpa ushauri.

" unaifahamu kiundani kidogo hiyo familia?.

" Familia gani?.

" Ya mzee edwad?.

" Mimi namfahamu huyo mzee edwad na huyo ndugu wa mama shakira ambae ni mke wa huyo mzee.

ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

BLOG