Search This Blog

Saturday, February 26, 2022

GENGE - 1

  

IMEANDIKWA NA : PATRICK CK

********************************************************************************

Simulizi : Genge 

Sehemu Ya Kwanza (1)


JULAI 15, 1991 DIAMOND JUBILEE


SAUTI KUBWA YA MUZIKI ilisikika kutoka katika ukumbi huo maarufu jijini Dar es salaam, katika kitongoji maarufu cha Upanga. Ni harusi ya kukata na shoka, kati ya Bi. Egra Mwakasimba na Dastani Kihwelo. Mamia, kama si maelfu ya watu waliujaza ukumbi huo. Wakila na kunywa huku wakitunuku zawadi kemkem kwa maharusi hao. Mishale ya saa mikononi mwa waliowengi ilioneshas saa sita kasoro robo usiku. Wenine walisaanza kusimama na kuondoka wakati wimbo huo unaojulikana kama ‘Wifi twende nyumbani’ ukirindima. Maharusi nao walikuwa wima wakitembea kwa mwendo wa maringo na hatua za hesabu kulielekea lango kuu, tayari kwenda kula fungate.

Nje ya ukumbi huo, gari la maharusi lilikwishaandaliwa na kuegeshwa mahala pake. Mercedes Benz E Class,jipya kabisa, toleo la 1990 lilipambwa likapambika. Gari hilo la pesa nyingi lilitolewa zawadi na idara ya Usalama wa Taifa ambapo Dastani Kiwelo alikuwa mwajiriwa mtiifu. Baada ya kuagana na ndugu na marafiki, Dastani, na mkewe Egra wakajitoma ndani ya chombo hicho kipya.

“Ooooh! Gari zuri sana mume wangu!” Egra akasifia mara tu baada ya kupokelewa na kiti cha ngozi laini. Akatazamana na mumewe na kubusiana kisha Dastani akapachika funguo mahala pake na kuliwasha. Ndani ya gari hilo walijiona wao tu, taratibu gari lile likaingia barabarani na kutokomea huku likiwaacha watu wakisindikiza kwa macho. Mazungumzo kati ya mtu na mkewe yalicukua nafasi wakati tairi zikichachafya Barabara ya Ally Hassan Mwinyi mara baada ya kuiacha ile ya Umoja wa Mataifa. Kutoka kwenye redio ya gari hilo, sauti ya mwaDanada Judy Boucher ilikuwa ikisindikiza kwa kibao matata ckinachokwenda kwa jina ‘Mr. Dream Maker’.

“Asante Dastani,” Egra akashukuru.

“Asante nawe pia, umenifanya niwe mwanaume sasa,” Dastani akamjibu mkewe huku akiongeza mwendo kulipita gari la mbele yake.

“Nataka tujenge familia ndogo, yenye upendo na furaha…” Dastani akajibu, alipotaka kulipita gari lingine akasikia honi kali nyuma yake. Akarudisha usukani kushoto na Benzi lile likatii amri. Mazda jekundu likampita kasi. Ndani ya Mazda lile ‘kibanda wazi’ kulikuwa na mwanamke mmoja ambaye ndiye dereva. Mshtuko wa wazi kwa Dastani ukaonekana.

“Vipi honey, mbona umepoa ghafla?” Egra akauliza.

“Hapana, hamna kitu,” akajikaza kiume, Waswahili husema.

“…unanificha, au ndo x wako? Wanaume amna wema!” Egra akalalama na kueukia upande wa pili.

Wanawake bwana! Hapo keshawaza mengine! Dastani akawaza na kupunguza mwendo. Kama mwanausalama, alishajua nini kitatokea kama akiendelea kufuata barabara hiyo. Akili ilimtuma kuchepuka na kuingia kulia kwenye barabara ndogo ya Kaunda, hakufanikiwa.

Kutoka nyuma ya kiti chake aliisi kitu chenye ncha kali kikimchoma pembeni kidogo ya uti wa mgongo. Akatulia huku gari likiendelea kuseleleka taratibu. Egra akaundua hilo, akageuka nyuma na kukutana macho na mtu aliyevaa soksi jeusi kufica uso wake. Alipotaka kupiga kelele akajikuta akipiwa na kiganja kigumu upande wa nyuma wa shingo, akazirai.

“Endelea na barabara hiyo hiyo mpaka nitakapokwambia,” sauti nzito ya mtu huyo ikamwamuru. Dastani akuwa na ujanja, akatenda aliloambiwa na mtu huyo. Kicwani mwake aliendelea kutafakari na kujaribu kukumbuka ni wapi aliisikia sauti hiyo, asipate jibu.

Dakika mbili zilizofuata walifika eneo la Mbuyuni.

“Kunja kushoto!” akaamriwa. Naye akatii na kucuku barabara ya Ruhinde. Mbele kidogo akatakiwa kukunja kulia, akafanya hivyona kuingia Mtaa wa Galu. Mara tu baada ya kukunja ile kona akaliona lile Mazda jekundu limeegeshwa kando.

“Simama hapo!” akaamriwa, naye akatii. Kutoka kwenye vivuli vya miti, wakajitokeza watu wengine watatu, wanaume ambao sura zao alizifahamu vyema. Dastani akateremshwa garini na kusimama chini,

“Umependeza Dastani, suti ya gharama uliyovaa, gari ya kisasa uliyopewa zawadi na wadosi wako… vyote ni kwa sababu ya kutuuza swahiba zako,” mwanaume wa makamo alizunumza huku akiwa kasimama mita chache tu kutoka kwa Dastani.

“Ilikuwaje ukakiuka maagizo Dastani, ata ukasababisha mipango yetu kwenda fyongo? Mpiganaji wetu , komandoo Salimu Manumba akauawa… yote kwa sababu yako. Na wewe mwenyewe kwa mkono wako ukamuua Bambross pale Embassy Hotel, ukachukua nyaraka nyeti na kuwapa mabosi wako. Tulijua u mwema, kumbe fukufuku mchangani. Watu wa aina yako uwa hawastahili kuishi… kwa taarifa yako, ulichokisema kwa mabwana zako ni asilimia kumi tu ya mpango mzima. Usifikiri tulikuwa wajinga kwamba tungeweka kila kitu mbele yako, la hasha! Sasa wewe utakuwa sanduku letu,” yule bwana akamaliza na kuingia kwenye lile Mazda jekundu pamoja na yule mwanamke wa Kizungu. Dastani akarudishwa garini mwake, mara hii, kwenye kiti cha nyuma huku vijana wengine wawili wakikaa upande huu na ule. Egra akiwa bado kwenye mzimio.

Safari yao iliishia Msasani Peninsula, kando kabisa ya Bahari ya Indi kulikuwa na nyumba moja pweke, ya kifahari. Ni katika nyumba hii ndipo, Dastani na mkewe, Egra, walikuwa wakielekea tayari kwa kuuanza usiku wa kwanza kama wanandoa.

“Usiwe na wasiwasi Dastani, fungate mtakula kama kawaida, na mtainjoi harusi yenu ndani ya nyumba ni hii hii,” yule bwana akazungumza. Dastani hakujibu. Yule mwanamke wa Kizungu mwenyue Mazda jekundu akaja na ndoo ya maji mkononi na kummwagia Egra. Egra akakurupuka na kuanza kuhema kwa nguvu na haraka haraka huku akimwita Dastani kwa sauti kali. Makofi mawili aliyozabwa na yule mwanamke yakamnyamazisa na kumwacha akitweta. Dastani, alilishuhudia tukio lile, akauma meno kwa uchungu na hasira.

“Mwacheni mtoto wa watu msimdhuru, haya hayamuhusu…” Dastani akatamka.

“Hatuwezi kumdhuru huyu, hana hatia, ila ataishi na sisi mpaka Munguamchukue mwenyewe, na wewe, malipo ya kazi yako yamefika…” alipomaliza kusema hayo kikafuatia kipigo kikali kutoka kwa wale vijana. Dakika kumi, zilimwachaDastani akiwa chini, hoi bin taabani, kila alipokohoa alitokwa na damu kinywani. Egra alikuwa akilia kwa uchungu kwa kila alipokuwa akitazama kipigo anachoshusiwa mwenza wake. Wale vijana baada ya kumsulubu Dastani, wakamwacha pale chini na kufunua buti la lile Mazda, wakatoa madumu mawili ya petrol na kuinia ndani ya ile nyumba. Dakika tano baadae wakatoka na kumwaga mafuta yaliyobaki kwenye kibaraza na mengine wakalimwagia lile Benz. Haikupita dakika mbili , upande wa baarini ikawasili boti ndogo.

Vijana wawili wakashuka wakiwa wamebeba miili ya watu wawili; mwanamke na mwanaume. Awakuongea na mtu,wakapitiliza ndani ya nyumba ile moja kwa moja. Iliwachukua kama sekunde arobaini hivi, wakatoka.

“Tayari boss,” wakamwambia yule bwana aliyesimama kando ya Dastani. Akawajibu kwa kutikisa kichwa. Akawapa ishara ya kumbeba Dastani na mkewe, wakafanya hivyo na kuwapakia kwenye ile boti. Pamoja nao, wakafuatana na wale vijana wengine.

“Ash to ash!” akatamka yule mwanaume na kuitoa sigara yake kinywani kisha akaitupia pale kibarazani. Moto mkubwa ukalipuka na kuichoma ile nyumba na kuteketeza lile Benzi wakati wawili wale wakipotea mbali ndani ya Mazda lao.

“Mungu amlaze panapomstahili,” yule bwana akatamka.

“Jesca! Moja kwa moja uwanja wa ndege,” akaoneza kusema. Yule mwanamke aliyeitwa kwa jina la Jesca akaitika kwa kichwa.


* * *


2002 Januari


BRUSELS –UBELGIJI


Wingu zito lilitanda katika anga la jiji hilo, barabara zilifunikwa na kwa barafu na kusababisha baridi kali kwa wakaazi wake. Daima kipindi kama hiki cha miezi ya Desemba mpaka Februari, nchi za Ulaya hupitia katika kipindi hiki, winter.

Nje ya jengo refu lenye sakafu thelathini na sita, linalojulikana kama Tour des Finances, gari moja la kisasa aina ya Audi liliingia katika uwanda wa maegesho, chini ya jengo hilo, likiiacha barabara kubwa ya Royale inayokatiza pembezoni mwake.

Kutoka ndani ghorofa ya ishirini na tano, ndani ya ofisi moja nadhifu iliyosheheni vitabu na makabrasha anuai katika rafu zake zinazong’aa kwa polish safi, hatua za mtu anayeujongelea mlango zilisikika pasi na kificho. Zilipofika mlangoni hapo, zikakoma. Sekunde kumi na tano zilizofuata, mlango ukafunguliwa. Kipande cha mwanaume kikaingia ndani. Kabla hajawasha taa kwa minajiri ya kufukuza iza hafifu lililosababishwa na wingu lile; aliona taa ikiwaka yenyewe.akapiwa na mshtuko na kuwai kugeuka upande wa pili ambako kuna swichi nyingine ya kuongoza taa hiyo.

“Usiogope, ni ugeni tu wa kawaida…” sauti ya mwanaume ikasikika upande ule. Yule bwana akashikwa na kigugumizi na kutazamana macho kwa macho na huyo aliyejiita mgeni.

“Wewe ni nani? Na unafanya nini katika ofisi yangu?” kile kipande cha mtu kikauliza uku akivuta kiti na kuketi nyuma ya meza yake kubwa.

“Mimi ni mgeni wako kutoka katika nchi iliyokulea, mpaka ukawa mtu mzima na kuiasi,” yule mgeni akajibu.

“Nani aliyekutuma?”

“Mama yako!” yule mgeni akajibu huku akicezea vidole vyake.

“Hivi ninyi Watanzania mna matatizo gani? Kwa nini ampendi watu wastarehe na maisha yao? Kutwa kucha mnatufuatilia, tuacheni!” akang’aka yule bwana.

“Jiulize! Ni Watanzania wangapi wanaisi Ughaibuni tumekuwa tukiwafuatilia? Kama si wewena washenzi wenzio tu… mngekaa kwa amani kama mngeondoka kwa amani…lakini mlichokifanya mnakijua, na adabu yake mnaijua. Nyote lazima muitumikie adhabu yenu…” yule mgeni akaeleza. Ndani ya mfuko wa ndani ya suti yake akachomoa bahasha ya khaki, juu ilikuwa na mhuri wa serikali.

“Ichane, uisome, nimetumwa na mama yako kukuletea…”

Yule bwana akaichana kwa kitete huku akivuta kamasi jepesi kulirudisa ndani ya pua zake ndogo. Akatulia kuisoma. kijasho chembamba kikamtiririka ilhali ofisi hiyo ilitawaliwa na baridi.

“Wewe ni nani?” akauliza kwa sauti huku akizungusha kiti kumtazama mgeni huyo. Mkono wake wa kuume ukabonyeza kitufe Fulani na kuruusu saraka ya siri kufunuka katika meza hiyo. Akabaki kakodoa macho akiwa haelewi nini cha kufanya.

“Usihangaike Bwana Titus Mwakibinga, bastola yako ninayo, nilikwisaichukua kitambo!”

Yule mgeni akamwambia mwenyeji wake ambaye mara hii alimtaja kwa jina la Titus Mwakibinga. “Umeju-aje ma-ha-li bastola ya-ngu i-li-po?” Titus akauliza kwa kigugumizi uku akipiga ngumi mezani.

“Kwani wewe ulifikiri hapo ni mahala pa siri? Mimi nilisapajua zamani sana, na sikupata tabu kuichukua,” mgeni akajibu.

“Nakuuliza kwa mara ya mwisho… wewe ni nani?” Titus akatupa swali uku akiwa amefura kwa hasira.

“Naitwa Amata Ric, au Kamanda Amata, TSA 1, code 005…” yule mgeni akajitambulisa huku tayari bastola ikiwa mkononi mwake. Titus alipotazamana na bastola ile alijikuta akiisiwa nguvu.

“Mbiyo za panya! Titus, hata kama kosa umelifanya mwaka ’82, hukumu iko palepale. Kama ulifikiri ukitoroka ndiyo utaukwepa mkono wa sheria, basi umeula wa chuya kwa uvivu wa kuchagua. Hukumu ya kesi yenu ilisomwa mwaka 1985, Desemba 28 na Jaji Antoni Mzavas. Wenzi wako walihukumiwa kifungo lakini wewe na wengine wachache mlitoroka nchi. Titus Mwakibinga, umehukumiwa kifo…” Kamanda Amata akamwambia pasi na lepe la tabasamu usoni mwake.

“Mimi sihusiki, serikali imenionea tu,” Titus akalalama.

“Sasa nani anahusika kama si wewe?”.

“Sijui!”

“Hujui? Kama hujui, basi ni mhusika mmoja wapo…” Amata akasema.

“Nooo!” Titus akang’aka mara alipoona bastola ile imeondolewa usalama.

“Kijana, nitakupa pesa nyingi sana,” akasema Titus.


ITAENDELEA

GENGE

EP2


Nooo!” Titus akang’aka mara alipoona bastola ile imeondolewa usalama.

“Kijana, nitakupa pesa nyingi sana,” akasema Titus.

“Sihitaji pesa yako, nimekuja kutekeleza kile nilichotumwa kama ulivyosoma kwenye hiyo hati,” Amata akasema na kumfanya Titus ageuke kutazama mezani. Macho yake yakagonganana neno KIFO, lililoandikwa kwa wino mzito na kupigiwa mstari mwekundu.

“Buriani Titus! Ukishakufa uwatokee wenzio kwenye ndoto uwaambie kuwa nitamuua mmoja baada ya mwingine. Popote watakapokimbilia…” Amata akasema. Kabla Titus hajaongea chochote tayari, risasi moja kutoka kwenye bastola yake mwenyewe, Glock 23, ikatoboa paji la uso. Titus Mwakibinga akajibamiza kitini na kichwa chake kuegemea kushoto. Amata akaipachika bastola ile mkononi mwa marehemu.

Nje ya jengo lile, akatembea taratibu huku mikono ikiwa mfukoninabubblish ikiteketea kinywani mwake, akapita barabara ya Royal kuelekea Best Western Hotel ambako ndiko aliwekeza makazi yake kwa muda akiwa katika operesheni hiyo. Ze Sindiket…


* * *

Ndani ya hoteli ile, Amata alijitupa kitini, akavua glovesna kuziweka juu ya meza ndogo ya kusomea. Akavuta kabrasha lake na kupekua hapa na pale akitazama kinachofuata. Alipojiridhisa na kazi yake akalikunja kabrasha lile na kulitia mkobani.

1981


DAR ES SALAAM


UPEPO MWANANA uliendelea kuvuma. Dirisha kubwa katika moja ya nyumba nyingi katika eneo la Kawe Mzimuni, liliruhusu upepo huo uwafikie wapendanao wawili waliokumbatiana kitandani usiku huo. Muziki laini kutoka katika santuri ya Mbaraka Mwishehe ulikuwa ukiendelea kusikika kwa sauti ya chini. Kelele za mibweko ya mbwa ikamshtua mwanamke aliyelala kitandani hapo. Mwanamke wa Kizigua, mwenye shepu isiyosemeka, akajivuta na kunyoosa mkono wake mpaka sehemu Fulani, uvunguni mwa kitanda hicho. Taa kubwa ya nje ikawaka na kufanya nuru kali ambayo kila kitu kingeonekana.

Mbwa waliendelea kubweka, mwanamama yule akaamka na kukiacha kitanda. Umbo lake la Kitanga likafanya mitetemo ya kuvutia na kuuweka dhahiri shahiri uanamke wake. Akakiacha cumba na kuelekea sebuleni. Wakati mbwa wakiendelea kubweka, mara kelele iliyofanyika kwa mawe matatatu kurushwa batini, ikamshtua mwanaume aliyelala kitandani hapo.

Akaamka na kupapasa upande aliokuwapo mkewe, hayupo. Akajiinua na kuketi kitandani. Nukta hiyo hiyo mkewe akainia chumbani humo na kujitupa kitandani, akavuta suka na kujifunika mwiliwe akikiacha kichwa tu nje.

Yule mwanaume akatoka kitandani na kuchukua shati lake kutoka kwenye henga. Akavuta hatua na kuelekea sebuleni, kasha geti kubwa. Akatoka nje. Nje tu ya geti hilo kuliegeswa Land Rover 109, na vijana wawili walikuwa wameliegemea.

“Vipi kwema?” akawauliza bila kuwasabahi.

“Mr. Chameleon!” mmoja wa wale vijana akatamka, akashusa kiko chake na kukimata vizuri kwa mkono wake wa kulia, “usiku kama huu, hakuwezi kuwa na wema. Twende zetu ofisini, kuna ujumbe wako.

“Oh shit! Hebu niacheni nipumzike na mama yenu kwanza ee!” Chameleon akajibu.

“Ni kweli mzee, ila huna budi kufanya hilo, namba moja anakuhitaji haraka,” yule kijana akamwambia Chameleon. Mzee yule akajishika kiuno, baada ya tafakari ya sekunde kama kumi hivi, akawaaca wale vijana na kuinia ndani. Mkewe alikuwa tayari keshalala fofofo. Dakika kumi zilizofuata, tayari alikuwa ndani ya Kaunda suti. Akamsukasuka mkewe na kumwamsha.

“Aaaa unanikatisha ndoto yangu bwana!” mkewe akasema huku akiamka na kuketi.

“Mi natoka…”

“Unaenda wapi?” akamuuliza mumewe.

“Kazini mara moja!” Chameleon akajibu.

“We na kazi zako, nisakuzowea. Siku hizi hata ndoa hatufaidi, naachwa na kiu tu…” akalalama mwanamke wa Kizigua.

“Usijali mpenzi, ngoja tulitumikie taifa,” akambembeleza.

“Haya nenda kwenye taifa lako unalolipenda ukalitumikie… na taifa hili unaloliacha likivamiwa na waasi usilalamike!” Mkewe akasema. “Aaaaa mama watoto, unafika mbali sasa…”

“Piiiiiiip! Piiiiip!” honi ya gari ikamshtua.

“Haya mammy, tutaonana baadae!”

“Sawa Daddy”.

Wakabusiana, na mzee huyo akaiacha nyumba na kuondoka zake.


* * *

Saa saba usiku, Chameleon alifika Msasani kuliko na makazi ya Rais ambaye wao walimtambua kama ‘namba moja’ kwa kuwa ndioye aliyekuiwa na dhamana ya ulinzi kwa nchi nzima. “Pole!” Rais akamwambia huku akimkaribisa kiti katika ofisi yake ndogo. Ndani ya nyumba hiyo.

“Asante Meshimiwa, nimeitikia wito…” Chameleon akajibu kwa adabu zote.

“Nisichukue muda wako mwingi… kuna taarifa hii hapa ambayo imenifikia jioni ya leo. Sikuifanyia kazi kwanza, kwa sababu nilikuwa naipitia kwa kina,” akamwambia huku akimkabidhi ile karatasi iliyoandikwa pande mbili. Chameleon akaipokea na kuisoma mara kadhaa. Alipomaliza, akaiweka mezani na kumsogezea mkuu wa nchi.

“Kwa hiyo, hata waziri Kibwana Mtokambali anahusika?” Chameleon akauliza.

“Ningekuwa na majibu, nisingekuita. Nataka ufanye uchunguzi… umchunguze waziri

Kibwana na nyendo zake zote. Pia nataka unipe taarifa kamili za hawa maafisa wa jeshi, akiwamo Kepteni Vincent Mwanachia,” Rais akamwambia Chameleon. Naye akajibu kwa kutikisa kichwa juu chini.

“Chameleon, this is confidencial… hakikisha, ndani ya siku mbili, unanipa majibu stahiki,” Rais akasema na kuagana na mwanausalama wake anayemtegemea. Chameleon alitoka ndani ya ile ofisi, akachukua na ile karatasi huku kichwa chake kikiwa kimejaa mawazo ya nini cha kufanya dhidi ya hicho alichoambiwa. Alitazama saa yake, ikamwonesha kuwa ni saa tisa kasoro robo usiku. Akafikiri aende nyumbani kuendelea kuumaliza usiku na mkewe, au aende ofisini kuanza kupana na kupanua juu ya hicho alichoambiwa, akupata jibu. Mawazo yake yakamrudisa kwenye kauli ya mkewe ambayo iliuchoma moja kwa moja moyo wake, ‘…na taifa hili unaloliacha likivamiwa na waasi usilalamike!’

Saa tisa na dakika na dakika tano usiku alikuwa akipita Barabara ya Chole, Masaki akiwa bado ajui sawia ni wapi aelekeako. Katika barabara hii kulikuwa na nyumba kadhaa za vibopa na vigogo wa serikali. Kati ya nyumba hizo, ilikuwamo ya waziri Kibwana Mtokambali. Bwana Chameleone alikuwa na tatizo kubwa moja, akishapewa kazi basi akili yake uwa hailali mpaka kazi ile itimie. Katika barabara ya Chole maeneo ya Oysterbay, Chameleone alikuwa akiendesha moja ya magari yao ya siri katika idara ya Usalama wa Taifa, Volvo. Alipokuwa katika lindi la mawazo, akautuswa na mwanga mkali wa taa za gari lililoingia katika barabara hiyo kutokea ile ya mbele yake. Akapunuza mwendo na kususa ukali wa taa zake, lakini lile ari la mbele yake alikufanya hivyo na kupelekea mwanga ule kumuumiza machoni. Akapunuza mwendo na kueesa kando kidoo akisubiri ari lile lipite. Badala ya kupita, likawasa indiketa ya kulia na kuinia kwenye ujia mfupi ulioishia kwenye lango la nyumba nyumba moja kubwa.

Bahati gani ya mtende kustawi jangwani? Gari lile lilisimama mbele ya nyumba ya mheshimiwa Kibwana Mtokambali. Chameleon akarudisha gari barabarani nakupita pale polepole akiendelea nasafari yake. TB 620, namba za gari zilisomeka namna hiyo. Kwa kamera yake ndogo ya Kirusi aina ya Cimena, akapiga picha lile gari kwa upande wa nyuma likiwa linamalizikia kuingia ndani ya wigo ule. Chameleon, hakuelewa kama gari lile, usiku ule, alikuwa waziri Kibwana mwenyewe akitoka mizunguko au mgeni kaja kumtembelea, hakuna jibu. Akaamua kuegesha gari lake kwenye kona moja mbele yake. Kisha akaamua kurudi kwa miguumpaka usawa wa nyumba ya waziri Kibwana, mwenye dhamana ya ulinzi wa nchi yake.

Ukuta ulioizunguka nyumba hiyo ulikuwa mrefu kiasi, kadiri ya mita tatu hivi na juuye kulikuwa na waya uliozungushwa kwa usatadi mkubwa na kibao kilichosomeka ‘DANGER’ chenye rangi ya njano na maandishi meusi kilining’inia. Akasimama nje ya ukuta huo kwa kuwa mazunumzo ya awali ya maamkiano ya watu hao aliyasikia.

“Hakuna mtu nyuma yako? Maana hii nchi unaijua!” Sauti ya Kibwana ikasikika.

“Aaaa naijua kazi yangu mheshimiwa…”sauti ya pili ikajibu. Chameleone hakuweza kuigundua sauti hiyo kuya ni ya nani. Alichokifanya ni kutega masikio kwa nguvu zote kusikiliza kile kitakachozungumzwa hapo nje.

“Enhe!”Kibwana akaendeleza mazungumzo, ambapo sasa dhahiri shahiri,sauti zao zilikuwa za chini sana.

“Kule kila kitu kipo sawa. Kesho, kijana wetu atafanya maandalizi ya mwisho na wale kuruta wamejiandaa vyema…”

“Mmeshawapa pesa?” Kibwana akauliza kwa kimuhemuhe.

“Tumewapa nusu na nusu nyingine baada ya kazi…”mgeni akajibu.

“Sawa, sasa sikiliza…”

“Enhe!”

“…mpango ubaki vilevile, saa na siku iwe ile ile… Mimi kama nilivyokwambia, kwa kuwa ratiba ya Mzee ninaijua vyema, nitawaambia ni wakati gani mzuri…”Kibwana akasema kwa msisitizo.


“Sawa,we unachotakiwa utuambie masaa sita kabla!” yule mgeni akajibu.

“Sawa, sasa mipango mingine, we pita ofisini kesho kama saa nane hivi!” Ukafuatia ukimya kidogo na baadae milango ya gari ikasikika ikifungwa. Chameleone akajibanza palepale na kulisuudia lile gari likitokomea katika barabara za Masaki.

Hapa kuna jambo kubwa! Akawaza na kujitoa katika ule ukuta. Akaliendea gari lake na kuingia ndani. Mara baada ya kushusha pumzi ndefu, akawasha injini na kuamua kurudi nyumbani kwake kujipanga kwa siku inayofuata.



SIKU ILIYOFUATA


Siku hii haikuanza vizuri kwa wakazi wa jiji la Dar es salaam.mvua kubwa yenye radi kali ilikuwa ikinyesa. Mzee Chameleon akajikuta anashindwa kubanduka kutoka katika kifua cha mkewe. Joto mujarab la mwanamama huyo lilimfanya alale kama motto kitandani hapo.

“Mwenzetu we huendi kazini?” Mkewe akauliza. Chameleone akainua saa yake mezani na kutazama. Loh! Ilikwishatimu saa tatu za asubuhi. Akakurupuka na kuijiweka tayari. Baada ya chai nzito kutoka kwa mkewe, akaingia katika gari lake na kutia injini moto.

Katika taarifa ya siri aliyopatiwa jana yake na Mkuu wa nchi, kulikuwa na orodha ya majina kadhaa ambayo kwayo ilimpasa kuyafatilia. Akiwa na mawazokichwani mwake, alijitahidi kuendesha gari kwa uangalifu. Akaiacha barabara ya Kawe na kukunja kushoto kuifuata ile ya Bagamoyo kuelekea Mwenge. Mita chache mbele, akakunja kushoto na kutazamana na lango kuu la kuingia katika kambi ya jeshi ya Colito, Lugalo.Askari aliyekuwa lindo akalifuata gari hilo na kuuliza maswali mawili matatu, kasha akaliruhusu kuingia. Chini ya mwembe mkubwa, ndani ya kambi hiyo akaegesa gari lake na kuvuta hatua ndogo ndogo kuelekea katika canteen ya maafisa.

Hakukuwa na watu wengi, lakini pia hakupenda kukaa kiti cha peke yake. Hatua zake, zikamfikisha mbele ya meza moja iliyokaliwa na mwaDanada alievalia sare za jeshi. Cheo chake ca Kepteni kilijionesha pasi na kificho kwa nyota tatu zilizojipanga vyema mabegani mwake.

“Hujambo bibie?” akamsabahi na kumtupia tabasamu lenye bashasha. Yule binti aliinua sura yake na kumtazama Chameleone kuanzia juu mpaka chini.

“Salama, karibu!” akajibu, kasha akaendelea kuburudika kwa supu ya kongolo iliyokuwa mbele yake.

“Karibu baba, nikusaidie nini?” ni sauti ya mhudumu iliyomshitua kutoka katika kumtazama afande yule, kepteni wa kike.

“Nipatie kongolo na Pepsi Cola. Itakuwa shin’ ngapi?” akauliza.

“Shilingi kumi na mbili tu,” mhudumu akjibu.

“Pamoja na hii ya Kepteni Zuhura…” akaongeza kusema. Yule afande aliposikia jina lake likitamkwa, akainua uso na kumwangalia huyo alitajaye kwa mara nyingine.

“Shilingi kumi na sita tu,” akajibu.Chameleone akatoa noti ya shilingi kumi kumi, mbili, na kumpatia.

“Hizo shilingi nne ununue bofulo kwa ajili ya watoto,” akamwambia mhudumu, naye akashukuru huku akitokomea jikoni. Mara baada ya kumalizana na yule mhudumu, akarejesha macho yake kwa afande yule.

“Asante kwa ukarimu wako,” Kepteni Zuhura akamwambia Chameleone.

“Karibu. Hivi ndivyo wanaume tunavyopaswa kuwa, nitapenda kutembelea ofisini kwako kabla sijaondoka kambini hapa leo hii…” Chamelleone akamwambia Zuhura.

“Karibu sana, lakini bahati mbaya, mimi sina ofisi…”

“KIvipi?”

“Ofisi yangu ni uwanjani tu,” Zuhura akajibu.

“Unamaanisha nini, wakati cheo chako kinakutaka kuwa ofisini? Wewe si ni ofisa!” Chameleone akazidi kudadisi.

“Ni kweli, ila mimi ni mkufunzi zaidi kuliko kuwa ofisini,” akamjibu.


ITAENDELEA












GENGE

EP3


Unamaanisha nini, wakati cheo chako kinakutaka kuwa ofisini? Wewe si ni ofisa!” Chameleone akazidi kudadisi.

“Ni kweli, ila mimi ni mkufunzi zaidi kuliko kuwa ofisini,” akamjibu.

“Ooh, safi sana! Je naweza kujua ni mkufunzi wa nini? Kama hutojali,” mtu mzima, Cameleone akauliza.

“Mimi ni mkufunzi katika Sanaa ya mapigano ya ana kwa ana. Huwa nakuja kuendesha mafunzo haya kwa vijana walio katika Special Force,” Zuhura akajikuta anabwabwaja bila simile mbele ya Chameleone. Muda huo huo, staftahi yake ikafika, akaagana na mwanamke huyo kasha yeye akaendelea na kuitupia kinywani supu aliyoagiza. Dakika ishirini baadae, akawa tayari nje ya kantini hiyo ya maafisa, akivuta hatua taratibu kuelekea jengo la utawala.

Hatua zake ndefu ndefu zikamfikisha kwenye jengo hilo, ambalo juu ya ukuta kuliandikwa jina Colito. Akasimama kwa sekunde kadhaa kabla ajaingia katika ofisi hiyo ambayo kwayo, mkuu wa kikosi hicho huwapo.

“Shida!” sauti kutoka nyuma yake ikamgutusha.

Chameleon akageuka taratibu ma kumtazama huyo asemaye. Kijana mmoja, mrefu, aliyependeza katika mavazi yake ya kijeshi, mgongoni mwake alikuwa kabeba bunduki kubwa, AK47. Kijana yule alikuwa kasimama imara, hacheki wala hatikisiki. Chameleon akajua wazi kabisa kuwa anasubiri jibu hata kama hajauliza.

“Aaaann nahitaji kumuona, Kepten Baka Baka,” Chameleone akajibu huku akisimama sawa kutazamana na mwanajeshi huyo.

“Bakabaka ndiyo nani?” yule mwanajeshi mwenye cheo cha Koplo akamtwanga swali Chameleon lakini hakujibiwa.

“Ninyi ndiyo tunaowatafuta, yaani tumewapiga kule kwenu Uganda lakini bado mnaendelea kutufuatafuata, sasa leo umejileta.

“Mimi nina shida zangu za ofisini kijana!” Chameleone akajieleza.

“Hakuna, wewe ni jasusi, umetumwa, sasa nakuweka ndani,” yule askari akasema pasi na mzaha. Sura yake tu haikuwa na chembe ya huruma, macho yake mekundu yalieleza wazi hisia zake za ukatili. Akapuliza filimbi iliyokuwa katika mfuko wake wa shati lile la kijeshi kwa mtindo wa pekee. Sekunde chache tu, wanajesi wenine wawili wakawasili.nao walikuwa katika kombati za jeshi, na mabega yao kuja katika viwiko yalivikwa kitambaa cheupe chenye herufi mbili nyekundu, MP yaani Military Police au kwa lugha nyepesi tungesema, polisi wa jeshi. Walipofika pale, yule bwana akawapa ishara tu, hawakuhoji, wakamchukua na kuondoka naye.

Mzee Chameleone akatupwa rumande maalumu ambayo huwekwa wanajeshi watukutu au wenye makosa mbalimbali. Na huwekwa ndani kwa amri ya wakubwa wao kulinana na kosa lenyewe. Lakini yeye aliwekwa humo kwa kutuhumiwa kuwa ni jasusi. Akaingizwa kwenye jengo moja lililojitenga kando kabisa na mengine. Kabla ya kufika katika jengo hilo walipita jirani kabisa na uwanja wa mazoezi na hapo alishuudia mazoezi makali ya Martial Art yakiendelea chini ya Kepteni Zuhura. Alipotazama upande ule, akagongana macho na mwanamke huyo aliyekuwa amesimama akiwatazama vijana wake.

“Songaaaa! Usiangalie wake wa wakubwa, ala!” Mp mmoja akamkaripia na kumsukuma mbele.

“Vua viatu, saa, mkanda, kofia na kama una pesa zote weka hapo kwenye mess tin,”akaamriwa, naye akatii. Alipomaliza kutekeleza hayo akaingizwa kwenye chumba kimoja ambacho ndani yake alikutana na watu wenine wanne. Watu wale wote aliwatambua kuwa ni wanajeshi kutokana na suruali zao za mabakamabaka. Ni yeye tu aliyekuwa amevaa kiraia, suti ya mtindo wa Kaunda.

“Kaa kwanza huko mpaka tutakapokuchukua kwa mahojiano…” MP mmojawapo akamwambia huku akimsukumia ndani na kuupia kufuli mlango huo wa chuma.

“Mzee, umepotea njia?” mmoja wa wale vijana akamuuliza.

“Nilipotea njia, nikajikuta ndani ya kambi, nikakamatwa na kuletwa huku,” akamjibu.

“Pole sana! Wananchi lazima muhesimu kambi na maeneo ya jeshi, na si kukatizakatiza kama mnaenda chooni,” akasema yule mwanajeshi.

“Sasa mbona aliyekuleta amesema usubiri kuhojiwa?” mwingine akadakiza swali.

“Mi sijui taratibu zenu za kijeshi, mi najua jeshi la wananchi, kwa hiyo sikuona shida kupita kuuliza niendako…” Chamelleone akawajibu na wote wakaanua vicheko.

Sekunde chache baadae, ukimya ukatawala kama mwanzo. Mzee Chameleone akiwa amekaa upande mwingine wa chumba kile, alikuwa kimya kabisa, akiwaza na kuwazua. Kwa namna nyingine alionakama amepewa nafasi ya utulivu ya kufikiri juu ya kile anachokifuatilia tofauti na anekuwa ofisini.

“We! Kwa hiyo… mi siwezi kukaa humu, ngoja nikaungane na wengine…” mmoja wa wale vijana wa jeshi akamwambia mwenzake.

“Unasema nini wewe? Mimi siwezi, kamwe, waje hata wakitaka waniue…” yule mwenzake akajibu.

“Wenzetu washakubali, wako nje saa hii…” akasema mwingine kabisa ambaye daima alikuwa kimya.

“Nimeapa kuilinda nchi yangu, na si vinginevyo!” akasema yule wa kwanza. Mara ukasikika mlango wa chuma ukifunguliwa. Yule mwanajeshi aliyesema hawezi kukaa mule ndani, akasimama haraka na kuuendea mlango wa chumba kile, kwa mikono yake miwili akasika zile nondo.

“Afandeee!” akaita.

“Tulia we muasi, wazalendo tupo kazini, kuilinda na kuipigania nchi yetu,” akajibiwa kutoka katika moja ya vyumba vile ambamo labda askari wale au yule aliingia.

Maneno yale yalimvutia sana Chameleone, akatega sikio kusikiliza kwa maana alishajuakuwa watu hao wanaongea kwa mafumbo. Dakika mbili baadae, akasikia michakacho ya miguu ya mwaDanamu anayetembea kwa hatua za haraka haraka kuelekea mlango ule. Wakati huo huo akamwona yule mwanajeshi pale mlangoni akaisogea nyuma kama sentimeta thelathini hivi. Kufuri likafunguliwa.

“Onana na Chatu haraka sana! Dakika kumi zikipita hujamwona, utarudi humu. Hakuna mwingine aliyechoka kukaa humu?” yule aliyefungua akauliza, huku akiwa anachungulia mule ndani. Macho yake yakagongana na ya Chamelleone. Sekunde mbili kama si tatu, akaingia ndani ya kile chumba.

“We raia vipi? Aliyekwambia hii ni selo ya watu kama wewe nani?” yulemwanajeshi akauliza.

“Selo ya raia iko wapi afande?” Chameleone akauliza.

“Atakujibu aliyekuleta!” akasema na kutoka nje huku akibana kufuli lile.

* * *

Baada ya saa sita kupita, Chameleone akatolewa ndani ya kile chumba na kuongozwa mpaka cumba kingine, akawekwa ndani yake na kutakiwa kusubiri hapo. Nusu saa baadae waliinia wanajeshi wawili. Mmoja alivaa kombati iliyopambwa kwa nyota tatu mabeani mwake na mwingine alivaa vilevile isipokuwa yeye alipambwa na v moja na kitambaa cheupe chenye erufi M na P. Yule kepteni akaketi kwenye kiti cha mbao na yule MP akasimama kando kiukakamavu kabisa.

“Wewe ni nani?” yule Kepteni akauliza. Chameleone akamtazama kwa jicho bay asana, hakujibu.

“Unajua hatupo kwenye utani ee, miaka hii nchi yetu imekuwa na maadui wengi sana. Taarifa niliyoipata ni kuwa wewe ni jasusi mmoja wa nchi hizo...”

“Hujakosea, mimi ni jasusi mmoja wa nchi hizo. Sasa siwezi kuzungumza chochote na wewe, namhitaji mkuu wako wa kikosi…” Chameleone akawaambia. Wale wanajeshi wakatazamana na kuanza kucheka.

“Unafikiri mkuu wa kikosi huwa anawasikiliza watu kama ninyi? Wewe tunakupia risasi kwa sababu umeidharau kambi,” yule kepteni akasema.

Ikawa zamu ya Chameleone kucheka, akacheka kwa sauti kubwa, kisha akanyamaza na kuwatazama.

“Nyie, msinifanye mimi mtoto mwenzenu, wewe mwili wako ushaingia risasi ngapi?” yule Kepteni hakujibu. Na Chemelleone akaendelea kusema.

“Kwa taarifa yako, hapa nilipo nina risasi mbili mwilini, hivyo siogopi risasi hizo unazozisema. Ondokeni hapa, mkamwite mwenye cheo cha juu kuliko ninyi wote…” akang’aka Chameleone. Yule kepten akasimama kutoka pale alipoketi na Chameleone akafanya hivyo.

“Mfundishe adabu!” akamwamuru yule MP, naye akamjia mzee yule akiwa tayari na mkanda wa jeshi mkononi, asijue anayemfuata kipumbavu ni nani katika medani ya upianaji. Hatua moja kabla ya kumfikia, yule MP akauzunusha ule mkanda hewani tayari kushambulia. Chameleone aliruka juu kimo cha ng’ombe, pio moja maridadi likamfanya yule kijana azunuke kama pia na kujibamiza ukutani, kisha akaanguka chini kama mzigo. Kepteni akamtazama yule mzee, kisha akamtazama kijana wake pale chini akiwa hana fahamu. Hakuwa na uamuzi mwingine zaidi ya kutoka nje na kuufunga mlango.

Dakika kama tano hivi wakawasili vijana wengine watano waliojazia miili. Wakafunua mlango wa kile chumba wakiwa na uchu wa kutoa kipigo kwa huyo mzee. Awakukuta mtu zaidi ya yule MPakiwa sakafuni. Hawakuamini, wakatafuta mpaka kwenye droo za kabati, hakuna mtu.

Wakambeba yule mwenzao na kumuwahisha hospitalini. Kishapo taarifa zaikafika kwa yule kepteni, hakuamini anachoambiwa. Akasimama kwa gadhabu na kutoka nje, alipofika mlangoni akakutana uso kwa uso na Chameleone aliyekuwa amesimama mkabala na ngazi za kuingilia katika jengo hilo la utawala. Palepale alipokamatiwa mwanzo. Yule kepteni akapatwa na mshtuko, hakujua nini afanye, arudi ofisini au aende kumkabili mzee huyo? Utata.

“Hivi, we mzee ni mzimu?” akamuuliza.

“Njoo unishike, uone kama mzimu una mifupa!” Chamelleone akajibu na kuanza kupanda ngazi.

“Unaenda wapi?” akaulizwa na yule kepteni.

“Ofisini kwako, tena uje bila kuchelewa!” Chameleone akamjibu na kumpita pale aliposimama, akaongoza na kuingia kwenye mlango wa tatu. Yule kepteni kwa woga akarudi ofisini kwake na kumkuta mtu mzima yule amekwishaketi kitini.

“Keti kijana! Kepteni Mwanachia…” akamwambia, na yule kepteni akaketi huku kicwani mwake kukiwa na mawazo lukuki.

Ni nani mtu huyu? Alibaki kujiuliza.

“Kepteni! Kumbuka kuwa hiki ni chombo cha wananchi, yakupasa kukitii kiapo chako, na si vinginevyo. Mbinu zozote chafuchafu kwa maslahi yako na ya wenzako, zitawagharimu maisha,” Chameleone akasimama na Kepteni Mwanachia naye akafanya vivyo hivyo.

“Wewe ni nani?” Mwanachia akauliza.

“Mzimu! Na usiku huu nitakutokea nyumbani kwako,” Chamelleone akamjibu na kutoka nje. Moja kwa moja akaliendea gari lake na kuondoka eneo lile.

* * *

Dakika thelathini baadae, Chameleone aliegesha gari lake nje ya ofisi yake ya siri, maeneo ya Hospitali ya Ocean Road, jirani kabisa naupande wa nyuma wa Ikulu ya Tanzania. Akaingia ndani na kuketi kitini, akiitazama meza yake iliyokuwa pweke muda wote. Kwanza akatua mezani hapo kabrasha alilotoka nalo garini, kisha akaingiza mkono mfukonina kutoa karatasi ndogo, ya rangi nyeupe iliyofifia, akaiweka kando ya kabrasha lile. Akainuka na kuuendea mtungi wa udongo uliokuwa kwenye kona ya chumba hicho. Ndaniye, akachukua Pepsi Cola moja kati ya sita zilizowekwa majini mtungini humo. Akafungua kwakutumia meno, na kurudi tena kitini.

Kilikuwa ni kibanda tu kikuukuu kilichotelekezwa pembeni kabisa mwa hospitali hiyo maarufu sana. Kama ungejaaliwa kukiona kwa nje basi ungesema ni ‘choo kibovu’. Hakikuwa na paa upande mmoja. Mbao zilizooza, ndizo zilionekana wazi waziwe. Upande mwingine kulikuwa na paa la vigae vikuukuu. Nje, pembezoni kidogo, palikuwa na mti mkubwa wa zambarau. Katika kibanda hicho, ndipo mzee huyu, mwanausalama mwaminifu wa serikali, alikuwa akifanyia mambo yake tofauti na ofisi yake ya kawaida ambayo huwa na wenzi wake wengi.

Akakisoma kile kikaratasi vizuri.


Bayankata itakuwa DDC Kariakoo

Usiku wa leo saa 4:00 usikose.

Mpenzio.



Hapo alikuta askari wa usalama barabarani pamoja na Landrover 109 iliyokuwa ikiifunga ari iliyopata ajali, tayari kuipeleka polisi.

* * *

Usiku huo huo, timu ya watu watano ilikutana katika nyumba moja kubwa huko Mtaa wa

Chole, Oysterbay. Mtaa unaokaliwa na watu wazito, hasa viongozi wa serikali. Ilikuwa huwezi kupita nyumba mbili bila kukutana na geti linalolindwa na polisi.

“Vipi?” Meshimiwa Kibwana Mtokambali akamuuliza Kepteni Mwanachia, aliyekuwa na watu wengine watatu.

“Inaonekana mipango yetu imegundulika,” Mwanachia akasema.

“Kweli kabisa,” akajibu mwanaume mwingine aliyekuwa na mawazo mengi. Waziri Mtokambali, akazunguka sebule huku na kule na aliposimama akawatazama wanaume wale.

“Tulisema mpango huu uwe siri, imekuwaje? Na mmejuaje kama umegundulika?” Kibwana Mtokambali akauliza huku akiketi kitini.

“Kuna mtu tulimkamata siku ya jana pale kambini. Nyendo zake hazikuwa zinaeleweka, tukamweka mahabusu. Baada ya kuhojiana naye, akawa anang’ang’ania kuonana na mkuu wa kikosi,” Mwanachia akaeleza. Macho pima, yakamtoka Waziri, aliyekuwa ndani ya pajama.

“Ukafanyaje?” akauliza.

“Aliondoka! Lakini majigambo yake yalinitia hofu…” Mwanachia akasema huku wenzake wakibaki kimya.Mheshimiwa Kibwana akatulia kimya kwa sekunde chache, kasha akamtazama Mwanachia kwa jicho la woga.

“Mnajua, hili jambo likimfikia Mwalimu, tumeumia. Lakini hapana, halijamfikia, kama ingekuwa limefika, basi mimi ningekuwa mtu wa kwanza kulijua,” akajifariji.

“Huyo mtu inabidi auawe haraka sana kwa kifo chochote kile… ama la, atatuharibia mipango na kitachofuata sote tutachezea kamba,” akaongeza kusema.

“Mkuu, jaribio la kwanza la kumuua limeshafanyika usiku huu…”

“Mmefanikiwa?” akadakiza kwa swali.

“Ametutoroka, gari yake imepondwa vibaya lakini hatujui ametutoroka vipi na wakati gani,” Mwanachia akaelezana kumwacha mheshimiwa Kibwana Mtokambali akiwa kinywa wazi.

“Chatu,” akaita. Mwanachia au kwa jina la kificho ‘Chatu’ akawa makini kusikiliza.

“Nabadili mpango, na naomba iwe hivyo…” akasema.

“Nakusikiliza mkuu,” akawa tayari kusikia.

“Maadam tulibakiwa na siku kidogo, naomba sasa huo mpango ufanyike kesho,” Kibwana akasema. Wageni wakatazamana, kasha wakarudisha macho kwa Kibwana Mtokambali.

“Sijasema hivyo kimakosa, bali kazi yetu iwe kesho kabla Mwalimu hajajipanga zaidi,” Mheshimiwa Kibwana aliongea mengi kwa lugha ya ushawishi na kila mmoja alikubali na kujiweka tayari. Mwingine alikuwa kiandika kila kinachojadiliwa mahala pale kwa ajili ya kumbukumbu za baadae. Walipomaliza wakapeana mikono na wakajiweka tayari kwa kazi. Wakaagana.

* * *

Usiku ule, mara baada ya kuiacha club ya DDC na kupita eneo la ajali, Chameleone alichukua kebu. Safari yake ilikuwa ya dharula kuelekea katika makazi ya Waziri Kibwana Mtokambali. Lengo kubwa lilikuwa ni kwenda kuifanyia upekuzi wa siri nyuma hiyo, usiku huo.

Hapa kuna jambo kubwa kati ya hawa maafisa wa jeshi na huyu waziri, lazima nipate jibu usiku huu! Akawaza akiwa ameketi kiti cha nyuma kwenye kebu hiyo. Akaitazama saa yake, “Ongeza mwendo kijana uniache Hospitali ya Ocean Road,” akamwambia dereva.

Dakika ishirini tu, akawa tayari ndani ya ofisi yake ya siri ambayo hata uingiaji wake hakuna mlinzi wa eneo hilo alikuwa akijua. Ndani ya ofisi hiyo hakutaka kupoteza muda. Alichukua vitu vitatu anavyovihitaji kwa kazi ya usiku huo. Nje tu ya hospitali hiyo alichukua kebu nyingine, moja kwa moja mpaka Mtaa wa Chole akashuka mbali kidogo na kuacha lile gari lipotelee mbali. Hatua zake, zikamfikisha usawa wa lango kuu la kuingilia katika jumba hilo. Asingeweza kupita getini kwa ulinzi ulikuwa hapo. Akazunguka ukuta mpaka pale alipojificha jana yake. Kwa mtindo uleule akaukwea. Kabla hajatimiza azma yake, akiwa tayari keshajitokeza kwa juu, macho yake hayakuamini yanachokiona. Gari lile aliloliona kule DDC, sasa amelikuta hapa pamoja na maari mengine matatu. Hili lilikuwa ni sadfa tu kwake, hakulitarajia. Kwa sekunde chache, ilimbidi kufanya majadiliano nahisia zake. Aingie kama alivyopanga au afanyeje? Hapana, haina haja, akapata jibu. Badala yake akatafuta eneo zuri ambalo linemwezesha kuona kinachoendelea ndani. Akapapata. Usawa wa dirisha la sebuleni. Ijapokuwa kulikuwa na pazia jeupe, zito, kulikuwa na nafasi kati ya pazia na pazia kama sentimita moja hivi, akazitumia. Akachukua darubini yake ya jicho moja na kuiweka tayari. Kupitia jicho lake la kulia akatumia sentimeta ile moja ya pazia kuweza kuona ndani kwa monocular ile ya Kirusia.

Naam, aliweza kumuona vyema Kibwana Mtokambali, waziri mwenye dhamana ya Mambo ya Nje. Hakuweza kusikia nini anaongea lakini alijuwa wazi kuwa kuna jambo muhimu linajadiliwa. Chameleone hakutapa kupoteza hata jambo moja. Amekosa sauti, akose hata picha? Haiwezekani. Alichukua kamera yake ndogo aina ya Cimena na kuiweka lenzi yake katika kifaa hicho. Akaweza kupata picha ya KIbwana Mtokambali. Wengine aliweza kupata picha zao wakiwa wanaagana na mheshimiwa huyo. Japokuwa picha hizo hazikuwa nzuri sana, lakini zilipatikana.Kwa haraka akakunja kionambali chake chenye jicho moja na kukitia mkobani. Tayari alimmaizi yule mmoja aliyeonekana kuwa ni karani wa kundi lile. Akazimezea mate karatasi zile, akiasubiri aone, kama zinahifadhiwa kwa mheshimiwa au zinaondoka na mtu huyo. Wale watu kule ndani wakaagana, karatasi zile, zikaondoka na yuleyule aliyeziandika. Chameleone, akajitoa pale ukutani na kuvuka barabara. Akajificha nyuma ya miti mikubwa huku akitazama magari yale yakitoka. Tayari alikwishajua ni lipi analolihitaji kati ya yale. Hakuwa na haraka, alifanya kazi yake kwa utulivu na kujiamini.

Gari la tatu, Datsun la buluu, ndilo alikuwa akiendesha karani wa kikao kile. Alipotupa jicho ndaniye, akatanabahi kuwa mtu huyo yu peke yake. Jambo jema zaidi ni kuwa, gari lile lilikuwa la mwisho. Akamshukuru Mungu. Kwa hatua za haraka akaingia barabarani na kukamata mlango wa nyuma wa Datsun ile, pick up. Akakwea kwa sekunde tatu tu na kutua ndani ya bodi hilo bila kufanya kishindo huku gari likiongeza mwendo. Safari ya gari lile ilikuwa ndefu, Chameleone aliendelea kuvumilia na kila alipoinua kichwa kutazama nje ya bodi lile, aligundua kuwa hakuna dalili ya kusimama.

Anaenda wapi? Akajiuliza huku akipiga moyo konde kusubiri mwisho wa safari hiyo.

Alipochungulia tena, akagundua kuwa tayari walikuwa wakipita uwanja wa ndege kuelekea Pugu. Akatazama saa yake, ilitimu saa kumi alfajiri. Lile gari likaanza kupunguza mwendo wake. Akajua muda wowote watasimama, akajiandaa kuteremka kwa upole kama alivyopanda. Naam! Mara tu baada ya kupita lango kuu la jeshi, kikosi cha wa wanaanga namba 603, lile gari likaiacha barabara na kusimama kwenye kichaka cha mikorosho. Mzee huyu alikuwa na akili nyingi sana mpaka nyingine zilimzidi. Alikuwa na uwezo wa kukusoma maamuzi yako ya dakika mbili mbele. Wakati Datsun lile likikanyaga udongo na kuingia kando kwenye mikorosho, yeye alikuwa tayari akining’inia katika mlango wa nyuma, akajiachia na kufika mchangani kwa utulivu. Kutokana na giza, hakuweza kuonwa na dereva, ukizingatia ilikuwa usiku. Akajificha nyuma ya moja ya mikorosho ile.

Ikapigwa honi mara tatu, ikatulia. Sekunde moja tu, aliibuka mtu kutoka upande ule wenye mikorosho mingi. Upande ambao kulikuwa na nyumba sita tu za jeshi. Na nyumba hizi ndizo chanzo cha jina Majumba Sita. Mtu yule , mrefu, mwenye mwendo wa kikakamavu, aliyevalia nguo za jeshi, alijitoma ndani ya gari lile. Chameleone akasubiri kuona kama kuna mwingine atajitokeza, hakuwepo. Alipotaka kujitokeza ili akaingie tena kwenye gari kwa mtindo uleule. Mlango ukafunguliwa na yule jamaa akateremka, akaagana na dereva na kupotelea kichakani. Lile gari likarudi barabarani taratibu na Chameleone hakupoteza muda, akadandia kama mwanzo. Safari ikaendelea. Dakika tano baadae, gari ikasimama mbele ya nyumba moja za jeshi, eneo la Banana, PMQ. Chameleone, tayari alikwishashuka na kujipenyeza uvunguni mwa pick up hiyo. Ijapokuwa ilikuwa na nafasi ndogo uvunguni, lakini alijitahidi kujisweka.

Yule bwana akateremka huku akipiga mruzi kufuatisha melodia ya wimbo mmoja wa Kisukuma. Mara baada ya kufunga mlango wa gari, akavuta hatua na kuingia ndani kwake. Chameleone akajito uvunguni na kujibanza kwenye kiambaza cha ukuta wa kuingia jikoni ambapo mtu yule alipita. Akatulia kuona hatua inayofuata. Taa za jikoni zikawashwa na dakika mbili baadae zikazimwa. Akasubiri kuona hatua nyingine ya mtu huyo. Dakika kama tano hivi akasikia maji yakimwagika chooni. Alilitegemea hili, kwa kuwa hakumwona mtu huyu hata nukta moja akienda kujisaidia. Utulivu ukaja, akajua sasa kumekucha. Akaufikia mlango akanyonga kitasa, akausukuma ndani. Upo wazi.

Wanajiamini sana! Akawaza akiwa anamalizia kuingiza kiwiliwili chake ndani, akaurudishia. Akaingiza mkono kwenye mkoba wake alioupachika vyema kiunoni, akachukua barakoa yake ya kuzuia gesi akaivaa. Mkono mwingine tayari ulikuwa umekamata chupa ndogo. Chupa ile ilikuwa na maandishi ya kikemia, CHCL3, basi. Haikuwa na maandishi mengine. Chameleone akaifungua na kuiziba kwa kidole chake. Akavuta hatua mpaka kwenye milango ya vyumbani na kuiruhusu gesi ile ifanye kazi. Akaoneza na kichupa kingine cha mtindo uleule. Watu wote walioivuta gesi ile, wakalala fo fo fo. Alipojiridhisha, akaingia chumba cha yule anayemtaka. Akamkuta tayari anakoroma tu, pembeni akiwa na mkewe aliyelala kihasarahasara, akiwa hana chochote mwilini mwake.

Ama kweli, ukiolewa, sharti ulale bila nguo! Akajisemea moyoni huku hisia za mwili wake zikipigana na dhamira, pepo. Mwanga wa taa za nje, ulimwezesha kuona yote haya. Katika droo kubwa, pembeni mwa kitanda cha yule bwana, palikuwa na zile karatasi, akazitazama zilivyolala, akazichukua na kufungua ndani. Zilikuwa mbili tu, zenye maandishi machache, akazisoma haraka haraka. Moyo ukampasuka kabla hata hajafika mwisho, muda unakwenda, akitweta. Alimtazama yule bwana pale kitandani, akatamani ambebe amtie garini na kumpeleka Ikulu kwa Rais. Haiwezekani, akatafuta karatasi mule ndani na kupata, akanakili yote yaliyoandikwa. Alipomaliza, akazihifadhi mkobani na kuziacha zile halisi. Akachukua kamera yake na kujaribu kuzipiga picha, ikiwa ni moja ya kuhifadhi kumbukumbu. Maana alijuwa akizichukua, atakuwa amewagutusha kwenye mpango wao dhalimu. Alipomaliza, akahakikisha ahachi alama nyuma yake. Akaondoka.


PAMBAZUKO


CHAMELEONE HAKUWA na furaha hata kidogo alfajiri hii. Tayari alikuwa amekwishaweka mipango yake vizuri. Mpaka dakika hiyo ni yeye tu aliyekuwa akijua nini kitatokea pindi pambazuko la siku hiyo likifika. Alitamani asimamishe saa,lakini hakuweza. Aliondoka kutpoka katika ofisi yake ya siri na kuelekea Msasani alfajiri hiyo. Breki zake zilimsimamisha mbele ya geti la makazi binafsi ya Rais ambako ni jana yake tu alikuwa hapa. Akateremka na kujitambulisha kwa walinzi. Wakamkaribisha na kuelekea ndani ya jumba hilo.




Breki zake zilimsimamisha mbele ya geti la makazi binafsi ya Rais ambako ni jana yake tu alikuwa hapa. Akateremka na kujitambulisha kwa walinzi. Wakamkaribisha na kuelekea ndani ya jumba hilo.

“Ila mzee hajaamka,” yule askari aliyekuwa akimsindikiza akamwambia.

“Usijali,” akamjibu huku tayari akiwa kwenye kibaraza, amezungukwa na askari takribani wane wenye silaha nzito. Kengele ya mlango ilimwamsha mfanyakazi wa ndani, akaufikia mlango. Akapewa taarifa hiyo, naye kadiri ya maelekezo yake ya kikazi akamwamsha mheshimiwa. Sebuleni hapo akabaki Chameleone na Rais tu. Saa kumi na mbili kasoro robo asubuhi.

“Mheshimiwa! Twende ofisini, kuna mambo ya kushughulikia haraka kabla ofisi hazijafunguliwa,” akamwambia.

Rais, akiwa ndani ya pajama, alikuwa kama aliyepigwa soti ya umeme.

“Ofisini?” akauliza.

“Ndiyo Mkuu! Tuna dakika tano tu, chukua vitu vya muhimu vya kutumia ofisini.

Ukishakamilisha hilo, utarudi kujiandaa,” Chemeleone akaeleza huku akianalia saa kila wakati.

“Sawa, wasiliana na watu wa itifaki ili taratibu za kawaida zifuatwe,” mkuu wa nchi akasema.

“Samahani kwa usumbufu, ila nipo kazini. Mkuu, unatakiwa kuondoka na mimi tu. Nataka nikakupe majibu ya kazi uliyonipa, haraka iwezekanavyo,” Chameleone akasema, mara hii kwa msisitizo zaidi. Kwa kusikia hili, Rais, hakuwa na ubishi. Kwa kuwa alikuwa akimwamini namba moja wake, akaingia chumbani na kutoka na mkoba mdogo. Dakika hizi chache, alivaa suruali na shati la kawaida tu. Wakachukuzana mpaka kwenye gari alilokuja nalo mwanausalama huyo. Askari walinzi walishtuka na kutaka kujua kulikoni Rais aondoshwe namna hiyo. Lakini yeye mwenyewe akawataka kutulia na kuendelea na ulinzi kama kawaida. Wakaondoka.

“Niambie kijana!” Rais akaanzisha mazungumzo.

“Hali ni mbaya mkuu, hutakiwi kuwa nyumbani wala Ikulu kwa sasa,” Chameleone akamwambia huku akiongeza mwendo.

“Umegundua nini?” akauliza.

“Huu ni mpango kabambe wa kukuondoa madarakani, kushindwa kwao mara mbili, wameona hakutoshi. Safari hii inaonekana wamejipanga kwa nguvu kubwa. Usiwe na wasiwasi hawataweza,” Chameleone akamtoa hofu mkuu wake.

“’Nini kinawasumbua? Umekwishajua?” akauliza maswali mawili kwa mara moja.

“Sababu hasa sijajua, ila nina hakika nitapata jibu tu, kwa kuwaninajua nani wakuanza naye,” Chameleone akamwambia huku akipunguza mwendo. Tayari alikuwa amewasili eneo la Magogoni, akaegesha gari ufukweni. Ilikuwa yapata saa kumi na moja alfajiri. Kutoka kwenye buti la gari, Chameleone akachukua jambakoti na kumvika mlindwa wake. Pamoja nalo, akamvika kofia kubwa, pama, iliyosukwa kwa miaa. Kisha akamwongoza mpaka kwenye mtumbwi mmojawapo kati ya mingiiliyoegeshwa ufukweni hapo.

“Ingia mzee, tunavuka ng’ambo!” akamwambia.

“Tunavuka na mtumbwi? Si tungechukua boti hapo polisi, mbona wako jirani tu!” Rais akamuuliza mwanausalama wake.

“Mzee, nahesimu mawazo yako, ila kwa sasa hayana nafasi.

Katika mtumbwi huu, walikuwa wao wawili tu. Safari ikaanza, Chameleone akapiga kasia kuelekea upande wa pili wa bahari. Mawimbi hayakuwa haba, yaliwasukasuka huku na huko lakini mtu mzima huyu alikuwa hodari katika kazi yake. Ukimya ulitawala, giza likatamalaki. Dakika thelathini na nne hivi, akaegesha mtumbwi huo pembezoni mwa bahari, upande wa pili, Kigamboni. Chameleone akamchukua mlindwa wake na kupita naye kwenye vichaka akikwepa kukutana na wavuvi na wachuuzi wa samaki. Mwendo kama wa dakika ishirini hivi kwenye vichaka vidogovidogo ukawatosha kuibukia katika barabara ya vumbi, mbali kidogo na bahari.

“Tunakwenda wapi hasa?” Rais akauliza.

“Tunakwenda mahali salama,” akamjibu huku akisimama na kumtaka mkuu wake asimame pia. Mbele yao kulikuwa na kitu kama kichaka kikubwa. Akavuta hatua mpaka pale, akapapasapapasa na kutengeneza upenyo mkubwa tu.

“Ingia twende!” akamwambia rais, na kuhakikisha ameinia kasha akarudishgia kama palivokuwa mwanzo. Akazunguka na kuingia upande wa pili. Lilikuwa gari. Gari dogo aina ya Beetle, au wengi waliliita kobe. Akalitia moto, akaliondoa eneo lile kwa kupita porini kwa porini kufuatisha njia nyembamba. Chameleone alipenda kulificha gari hilo mahali hapo kwa ajili ya kazi zake za siri au moja ya kujilinda inapobidi.

Safari yao ikaishia huko Gezaulole, katika nyumba ya ukubwa wa wastani, iliyojenwa kwa udongo na kusakafiwa vyema kwa saruji. Juu ilipauliwa kwa bati na kuzunukwa kwa uwa wa mianzi.

Chameleone akaegesha gari upande wenye korongo na kuifanya nyumba ile ionekane kwa juu. Wakateremka na kuingia ndani ya nyumba hiyo pweke. Haikuwa inakaliwa na mtu, lakini ilikuwa safi kuanzia nje mpaka ndani. Chumba kimoja wapo kiliteuliwa kumhifadhi mheshimiwa kwa muda. Kilikuwa kimetimia, redio ndogo, kitanda cha BANCO, mtungi wa maji baridi pamoja kiti kimoja.

“Karibu mafichoni mzee! Najua umeshtuka kwa yote niliyofanya lakini sikutaka kumhusisha mtu yeyote katika hili kwa sababu ya usalama wako. Kuna baadhi ya wanajeshi katika vikosi vyetu wameunda kikundi cha uasi. Ndani yao kuna makomandoo wawili na maafisa kadhaa ambao wameshiriki kikamilifu katika kumng’oa Amini. Unawafahamu vyema, japokuwa wachache huwajui. Wamepanga mpango kababe ikiwemo kuvamia Ikulu na kukufurusha mbali,” Chameleone akamweleza Rais.

Akampatia ile karatasi aliyonakili, na kumpa kama dakika kumi za kuisoma. Akaisoma na kuirudia mara kadhaa. Alipomaliza akaitua kando na juu yake akaweka bakora yake ambayo daima haiachi.

“Hakuna kingine, ni uroho wa madaraka… Afrika sijui tutaelimika lini! Wanataka kwenda Ikulu. Ikulu kuna nini? Ni matatizo tu na msongo wa mawazo siku zote, labda kama unataka kwenda na kutumia mali za Watanzania kwa manufaa yako…” akazungumza kwa ukali kidogo. Akatulia kimya klwa sekunde kadhaa. Akaomba karatasi na kalamu, akaandika ujumbe fulani wenye maneno machache tu. Akaikunja ile karatasi na kumpatia Chameleone.

“Mkabidhi waziri wa ulinzi,” akamwambia. Chameleone, akaipokea na kuiweka mfukoni.

“Mkuu, mimi ninakwenda kuona hali halisi ilivyo. Hapa ndani pana kila kitu. Nitarudi baada ya saa nne kukuletea taarifa kamili. Unaweza kupata kinachojiri kwa kusikiliza redio hiyo ndogo kwa sasa,” Chameleone akamwambia rais na kasha akatoka ndani ya nyumba ile. Akahakikisha milango yote imefungwa. Kwa kutumia njia zake za siri, akawasili pwani ya Kigamboni na kuvuka mpaka upande wa pili.

Jua la saa kumi na mbili na nusu asubuhi lilikwishaanza kulipendezesha anga kwa miale ya dhahabu. Chameleone alivuta hatua pembezoni mwa ukuta wa Ikulu, kandokando ya bahari kuelekea hospitali ya Ocean Road. Alipoizunguka na kuingilia mlango wa nyuma, akatokea kwenye ofisi yake ya siri, akaingia na kujifungia. Akachukua redio yake ndogo na kuiwasha, akatafuta idhaa ya taifa na kutega sikio kusikia nini kinaendelea. Kipindi cha Majira cha asubuhi kilikuwa kikiendelea.

Hakuna wanachojua hadi sasa! Akawaza. Hakuona haja ya kupoteza muda, akatoka na kupenya ndani kwa ndani mpaka katika jengo la Ikulu. Akawakuta watu wakiendelea na shughuli zao za asubuhi ikiwa na kuweka vizuri mazingira kwa kuwa hiyo ni ofisi ya rais. Akasalimiana na kupita moja kwa moja mpaka katika chumba cha usalama. Humu ndani alimkuta binti mmoja tu aliyekuwa akifuta vioo na kuweka kabrasha vizuri katika rafu zake.

“Selina!” akaita.

“Bee!” akaitika huku akigeuka kumwangalia mtu huyo. Akampa heshima yake na kusubiri kupata maagizo.

“Mwite Simbaulanga na James…” akamwagiza.

“James yupi?” Selina akauliza.

“James Msambamagoya,” akamweleza.

“Msambamagoya hayupo kazini, aliondoka jana usiku wa saa tano na hakurudi mpaka sasa,”

“Alisema anaenda wapi?”

“Alituambia tu kuwa ana dharula,” akajibiwa.

Chameleone akabaki kimya kwa sekunde kadhaa, kichwa chake kikawa kama kimepigwa shoti ya umeme.

“Ok, chukua hii barua, moja kwa moja ifikishe kwa Waziri wa ulinzi, kasha urudi hapa ninakuhitaji,” akamwambia mwaDanada huyo. Selina aliipokea ile bahasha na kuiacha ofisi hiyo.

* * *


BANANA BAR


James Msambamagoya aliegesha gari lake aina ya Ford Hungrier pembezoni kabisa mwa baa maarufu iliyojulikana kwa jina la Banana, karibu na kambi ya jeshi kikosi cha Wanaanga. Ndani ya gari lake alikuwa yeye na mtu mwingine, mwaume, mrefu, mweusi.

“Kama nilivyowaambia, hatutakiwi kukosea hata kidogo,” James akamwambia yule mtu.

“Hatuwezi kukosea hata kama tumefanya kwa uharaka. Simbamwene keshaenda Msasani kama ulivotuambia. Na nyuma yake kafuatiwa na wapiganaji mahiri endapo kutatokea rabsha yoyote,” yule mwanaume mweusi akajibu.

“Safi! Pale hatopata upinzani kwani waliopo ni polisi wa kawaida, hawajui medani za vita,” James akaongeza kusema.

“Halafu, kikosi namba mbili tayari kimeshafika Magogoni, na klila mmoja ameshachukua position yake,” yule mwanaume akaeleza zaidi.




Halafu, kikosi namba mbili tayari kimeshafika Magogoni, na klila mmoja ameshachukua position yake,” yule mwanaume akaeleza zaidi.

“Safi sasa, ngoja niwaone akina Mwanachia nijue nini kinaendelea…” James akamwambia yule mtu. Kisha akateremka garini na kufuatiwa na yule bwana.

Ndani ya baa hiyo kulikuwa na watu wane tu, waliojifungia katiak cumba maalumu. Mazungumzo machache lakini yenye unyeti yalikuwa yakiendelea.

“Mheshimiwa rais yuko tayari kuingia Ikulu, tayari amefika kwa mara ya mwisho katika ofisi yake ya zamani…” Mwanachia akalieleza jopo, “Chatu, kama tulivyopanga, mara tu tukishika hatamu, nafasi yako ni Waziri wa Ulinzi, utahakikisha majesi yote unayatiisha kwa masaa machache. Kumbuka kuwaweka tayari watu wetu katika kila kamandi,” akaongeza kusema.

Mjumbe mwingine akatazama saa yake. Saa moja na dakika sita asubuhi, “Jamani, mbona Tito hafiki?” akauliza.

Swali hili lilimgutua kila mmoja, hakuna aliyemaizi kuhusu mtu huyo kutokuwapo.

“Si kawaida, na kumbuka ni yeye mwenye dondoo za vikao vyetu, ni mtu muhimu, James , kabla hujakaa vizuri naomba umfuatilie huyu bwana ujue nini kimemsibu mpaka sasa hajafika,”

Mwanachia akatoa maagizo. Kwa kuwa kikao kilipokuwa kikifanyika na nyumbani kwa Tito Mwakibinga hakukuwa mbali, haikuwa vigumu kufika. James, mtumishi wa idara ya usalama wa taifa, mlinzi wa karibu wa rais aliondoka. Huyu ndiye aliyekuwa akitoa siri zote za Ikulu na mienendo ya rais ikiwamo ratiba zake za kila siku. Ni yeye aliyewaambia kuwa siku hiyo rais atakuwa nyuimbani kwake Msasani na si Ikulu. Ni yeye aliyewapa mpaka majina ya walinzi wa nyumba siku hiyo. Yeye huyo huyo ndiye alikuwa masterplan wa mchezo huu. Akiwa anajua fika nini kitatukia siku hii, aliiacha ofisi na kuaga kuwa ana dharula, akatoweka usiku.



MAKAZI YA RAIS, MSASANI


Jairosi Simbamwene, komandoo wa Jeshi la wananchi aliwasili eneo yaliyopo makazi binafsi ya rais. Akapita kando kando ya maua marefu kulielekea lango kuu la nyumba hiyo. Alitembea kwa kujiamini, pasi na wasiwasi wowote huku nyuma yake akifuatiwa na Jeep moja jeupe lililokuwa na wanajeshi, waliovaliovalia mavazi yao ya bakabaka. Vijana hao wote walikuwa na bunduki za kivita mikononi mwao. Hakuna aliyewashangaa, kwani eneo hilo kuwa na askari ni kawaida. Lile jeep lilikunja kona kali likitokea upande wa Kawe na kunyoosha kuelekea katikajumba hilo.

Walinzi wa nyumba ya rais, walijitokeza kulitazama gari hilo lililokuwa likija kasi. Mmoja wao akawahi kibandani ili kuweza kupia simu mahali salama. Hakufanikiwa. Komandoo Simbamwene, alitua ardhini kutoka juu ya kibanda kile. Pigo lake likatua kicwani mwa askari yule, akaenda chini. Kabla wenzake hawajafikiri cha kufanya, tayari alivingirika na kumtia nwara mwingine huku bastola yake ikikoroma na kumvunja mguu wa tatu. Lile Jeep likagonga geti na kukunja kona kali upenuni mwa nyumba ile. Vijana wa jeshi tayari walikuwa chini wamekwishawadhibiti walinzi katika kona zote. Wakawakalisha chini huku mitutu ikiwa vichwani mwao.

Komandoo Simbamwene, aliifikia sebule kubwa ya jumba hilo akiwa na vijana wawili wenye bunduki kubwa za AK 47. Moja kwa moja mpaka chumba cha Mkuu wa nchi, hakuna mtu. Wakasaka kila chumba , kila kona, kila banda. Hakuna mtu.

Kipigo kikaanza kwa walinzi kushinikiza waseme, lakini wote walikiri kuwa hawajui. Zaidi waliwaambia kuwa tangu wameingia lindoni hakuwapo nyumbani.

Dakika kumi zilizofuata, magari matatu yakiongozwa na pikipiki kubwa la polisi yalilikaribia lango la jumba hilo. Kwa uharaka wa ajabu, wale wanajeshi wakawaficha walinzi wote. Simbamwene akamchukua mmoja aliyekuwa naye ndani.

“Fungua geti, ole wako ulete hila yoyote nakufumua kichwa chako,” akamwambia. Yule askari akatembea haraka na kufunua geti. Yale magari yakaingia uwanjani na kukuta lile jeep limeegeshwa.

Ndani Benz ambalo daima upanda rais, alikuwa ameketi Simbaulanga na nyuma ya usukani kulikuwa na Chameleone. Magari mengine mawili yalikuwa na askari wenye silaha nzito. Walijua wanaenda kufanya nini, hivyo walikuwa tayari. Msafara uliposimama tu, vioo viliteremshwa na risasi zilianza kurindima. Kwa ustadi wa hali ya juu. zilikuwa dakika tatu za mabishano ya risasi. Vijana waliokuwa wakiongozwa na Simbamwene walidhibitiwa kikamilifu. Chameleone alishuka garini, bastola Smith and Wesson ikiwa imefumbatwa vyema katika kiganja cha kulia. Kwa uharaka na ujuvi mkubwa alijitupa katika maua na kutambaa kuelekea ukuta wa baraza ya nyumba hiyo. Alipoufikia, alisimama na kutembea kwa kunyata. Hatua kama nne hivi zilimfikisha katika mlango wa nyuma.

Akaupiga teke, ukafunguka. Bastola ya Simbamwene ikabanja, lakini shabaa aikuwa makini. Chameleone akajirusha chini kiufundi. Mara tu alipotua sakafuni, bastola yake ikakohoa. Risasi moja iliyoipita mtambaa panya ikakipata sawia kiatu cha Simbamwene. Aliporuka sarakasi akajikuta amechelewa. Maumivu makali yakapita kwenye unyayo wake. Akatoa tusi zito. Kwa kuchechemea, akamwendea Chameleone na kumuwahi kwa teke moja la mkono, bastola ikamtoka. Teke linguine, akalidaka na kumvuta mguu. Simbamwene aliona Chameleone anapigana kwa mbinu za kitoto sana. Akamdarau, akamkamataukosi wa Kaunda suti yake na kumuinua lakini mwanausalama yule hakumuachia mguu; akamng’ata. Simbamwene akapiga unyende na kumwachia Chameleone. Akasimama haraka, akainua kiti na kukirusha, kikatua kichwani mwa Simbamwene. Chameleone akaruka sarakasi na kuikamata tena bastola yake. Alipoinyoosha kupata shabaha, Simbamwene kwa weledi wa kushangaza, alichumpa na kupita kwenye kioo. Akaangukia kwenye maua nje ya nyumba. Risasi nne za Chameleone zikamkosa na kuchimba sentimeta chache kando ya dirisha.

Nje ya nyumba ile, Simbamwene, hakupoteza hata sekunde, aliruka sarakasi na kutua nje kabisa ya wigo huku akikoswakoswa na risasi za wanausalama. Vijana wake wote walikuwa tayari mikononi mwa serikali. Chameleone na vijana wachache wakatoka nje kumtazama komandoo huyo wasimwone.

“Hawezi kucheza na mimi!” Chameleone akamwambia Simbaulanga huku akiiweka vyema bastola yake. Walipotokeza nje kabisa, majirani wakawapa ishara kuwa ‘amekimbilia huku’. Simbaulanga na Chameleone wakachukua Honda kubwa lililokuwa limeegeshwa nje ya nyumba mojawapo. Mwendo wao wa kasi ukawafikisha katika barabara kuu itokayo Kawe kuelekea Kinondoni. Katika barabara hiyo ya vumbi, walimshuhudia Simbamwene, akimtoa kwa nguvu Mwarabu mmoja aliyekuwa na familia yake garini. Alipowaona wabaya wake, akamvuta mama wa Kiarabu na kumweka ngao mbele yake, na domo la bastola lilikuwa limegusa sikiole.

“Mkithubutu namuua!” Simbamwene akawaambia. Tayari Chameleone alikuwa kasimama chini na bastola yake ikimwelekea mtu huyo.

“Mwache huyo mama aende!” akamwamuru.

“Simuachi!” akajibu huku akimvuta kinyumenyume mpaka katika mlango wa gari.

Simbamwene, akapia risasi moja hewani na kumsukuma kwa nguvu yule mwanamke kuelekea kwa Chameleone. Chameleone akamkwepa na klufyatua risasi moja iliyopita kioo cha nyuma, sentimeta moja tu kando ya mwamba wa kushoto wa kioo cha nyuma. Simbamwene, mara baada ya kumsukuma yule mama wa Kiarabu, aliwahi kujitoma ndani ya gari, nyuma ya usukani. Kutokana na akili za mtyu mzima Chameleone alijua wazi nini komandoo huyo atafanya. Risasi yake ilipenya kisogoni na kufumua vibaya paji la uso la Simbamwene na kuchafua kioo chote cha mbele kwa damu na ubongo.

Chameleone bado alikuwa kasimama huku mikono yake ikiwa bado imelenga bastola upande uleule kana kwamba anasubiri mtu huyo ateremke. Akasonya na kushusha bastola yake taratibu.

“Amekwisha!” Simbaulanga akamwambia Chameleone.

“Yes! Nilikwambia hawezi kucheza na Chameleone.


WAKATI HUO HUO


Kambi ya Jeshi ya Twalipo


Waziri wa ulinzi aliwasili na kukaribishwa na mkuu wa kambi hiyo. Hali ya kambi haikuwa shwari. Mapinduzi.

“Nchi imepinduliwa?” yule Mkuu wa kambi akamuuliza waziri.

“Hapana, lakini nimekuja kwa kuwa nahitaji kukutana na vijana wako wanaohamasisha mapinduzi,” waziri akasema.

“Loh! Nahisi tu hawapo. Watu niliokuwa nawahisi, wote sijawaona kambini tangu jana usiku,” Mkuu wa kambi akajibu.

Kikao hiki cha siri kilifanyika ndani ya ofisi ya mkuu huyo. Baada ya mazungumzo mafupi, wakafika watu wengine watatu kutoka idara ya utambuzi ya usalama wa taifa. Tarumbeta la dharula likapigwa, askari wote wa vyeo vyote wakafika na kujipanga katika uwanja mkubwaunaotumika kwa gwaride. Lengo la waride hilo lilikuwa kwamba, yeyote ambaye hangekuwepo basi angehusishwa moja kwa moja na kadhia hiyo. Mtindo huohuo pia ukafanyika katika kikosi cha wanaanga Banana na kile cha Mgulani.

Orodha ya wasiokuwepo na vyeo vyao ikaandikwa, kasha vikapangwa vikosi vya ulinzi katika maeneo nyeti ya serikali. Ikatangazwa, yeyote aliyewekwa katika orodha hiyo, atakapoonekana popote akamatwe, ikiwa pia kuwatafuta popote walipo.

Waziri wa ulinzi akatumia pia muda huo kuitisha kikao na Mkuu wa majeshi na kebineti yake kuzungumza juu ya nini kimesukuma yote haya kutokea.




Waziri wa ulinzi akatumia pia muda huo kuitisha kikao na Mkuu wa majeshi na kebineti yake kuzungumza juu ya nini kimesukuma yote haya kutokea.

* * *

“… Dar es salaam. Komandoo mmoja wa jeshi la Tanzania ameuawa na askari wengine kumi na mbili kukamatwa leo asubuhi baada ya kurushiana risasi na wanausalama, katika jaribio la kutaka kuipindua serikali. Habari kamili juu ya tukio hilo tutawaletea hivi punde.

Wakati huohuo, Makamu wa Rais ametangaza hali ya tahadhari kwa wananchi kutotembea ovyo kama hauna shughuli maalumu…”

Taarifa ya habari kwa ufupi ya saa mbili asubuhi ilitangaza.

Waziri wa mambo ya nje, Meshimiwa Kibwana Mtokambali akainyanyua redio yake na kuirusha ukutani. Redio ile ndogo ikapasuka vipande viwili huku betri zake zikitawanyika huku na huko. Akatoa sonyo refu lililofuatiuwa na ngumi iliyotua juu ya meza na kuacha vitu visivyo na nguvu luparanganyika.

“Wanatuzidi wapi?” akauliza kwa sauti kana kwamba kuna mtu wa pili, kumbe la.

Kuchanganyikiwa. Siku hii ilikuwa ni tofauti kabisa na nyingine. Kwanza waziri huyu alifika mapema kazini kuliko hata katibu wake. Alivaa suti ya gharama sana aliyoinunua huko ughaibuni, maalum kwa siku maalum. Siku hiyo, ilikuwa hii. Kila mara alifanya mazoezi ya kutabasamu kama rais, kuketi na kujaribu kuongea peke yake kama rais. Loh! Asali ikageuka shubiri. Mtokambali hakukubaliana kabisa na kile alichokuwa anakisikia redioni.

“Kikosi changu hakiwezi kushindwa kamwe,” akajiapiza huku akisimama. Dakika hiyo hiyo, simu ya mezani ikaanza kuita kwa fujo.

Nani huyu? Akajiuliza. Akaukamata mkonga wa simu tayari kusikiliza, moyowe ukaanza kudunda bila mpangilio kama saa mbovu. Akasukuti kwa sekunde kadhaa, simu ile ikakatika.dakika moja baadaye ikaanza kuita tena. Kwa mkono ulojaa kitetemeshi, akauweka sikioni mkonga ule.

“Mheshimiwa, mipango imevurugika.

Yatupasa kukutana shimoni haraka iwezekanavyo,”

Sauti ya upande wa pili ikamwambia.

Bila kificho, aliielewa vyema sauti hiyo, Chatu. Akaushusha ule mkonga na kuuweka mahala pake. Akaanza kuchachawa. Hakujua nini anatakiwa kufanya. Alichoamua ni kuacha kila kitu na kuondoka. Alipoufikia mlango tu, simu ile ikaita tena, akasimama huku mkono wake ukiwa kifuani upande wa moyo.

Nani tena? Akajiuliza. Akarudi na kuinyakuwa simu, akaiweka sikioni.

“Unatakiwa kufika Ikulu haraka sana kwa kikao cha dharula…”

Toooba! Moyo wa Mtokambali ukapiga samasoti. Akazidi kuchanganyikiwa. Aende wapi? Shimoni au Ikulu? Utata. Akabaki katika mbutwaiko, katikati ya ofisi, akasimama kimya.

Nisipoenda Ikulu, nitakuwa nimejichongea, na vipi kama nikienda wakati wameshaijua hila zangu? Watanitia mkononi! Akawaza. Hata hivyo akajikuta hana la kufanya. Akatoka ofisini kwa mwendo wa kinyonge na kulifikia gari la ofisi, Land Rover 109.

“Nifikishe Ikulu,” akamwambia dereva na yeye akaketi kiti cha nyuma akiwa na mawazo.

* * *


Shimoni


Katika msitu wa Kazimzumbwi, watu nanne walikuwa wamekutana katika nyumba moja kuu kuu, katikati ya shamba kubwa sana. Sura zenye wasiwasi zilitawala. Hakuna aliyekuwa akiongea kati yao badala yake, kila mmoja alikuwa anaomba ombi lake. Ni mtu mmoja tu alikuwa hajafika bado, Mtokambali, ambaye mchana wa siku hiyo alitegemea kutangazwa ‘Mwenye Nchi’.

“Nini kimetokea? Wapi tumezidiwa?” Chatu akauliza kwa kuvunja ukimya.

“Hata sielewi, yaani sijui… Simbamwene kauawa!” James akasema kwa mshangao. “Najua ni nani aliyetibua mpango huu…” akaongeza kusema. Kwa maneno hayo, kila mmoja akagutuka na kumtazama mwanausalama huyo.

“Yupo kati yetu?” Mwanachia akauliza.

“No! hayupo kwenye cyndicate hii… ninachojiuliza ni wapi siri hii imevuja?” James akasema.

“Kwa sasa hatuna muda wa kujadiliana nani katoa siri au nani kafanya nini, mpango uliopo sasa ni sisi sote kutoroka nchi…” akadakiza mjumbe mwingine, na hapo kila mmoja akaunga mkono hoja kwa kutikisa kichwa.

“Mpaka sasa hatujui Mtokambali yupo wapi! Kapatwa na nini! Tulishakubaliana hili, na tukala yamini, kuwa mambo yakishindikana, kila mtu aitoroke nchi, tukakutane kwenye shimo jingine…” Mwanachia, mwanajeshi mwenye cheo cha kutosha, akawaambia wenzake. Kikao kikafungwa na ajenda iliyohitaji utekelezaji ni moja tu, kutoroka.

“Lakini tumeshindwa wapi?” mjumbe mwingine akauloiza kwa sauti ya chini.

“Hilo halina mjadala, kwa sasa yatupasa kutekeleza kilicho mbele yetu, basi… Siku ya kumi kutoka sasa tukutane pale ambapo mkataba waetu unasema. Asanteni na kwaherini!” Mwanachia akawaambia wajumbe na kikao kikafungwa.

* * *

Nchi ilikuwa kimya. Habari iliyotikisa kila kona ni juu ya kuuawa kwa komando Jairosi Simbamwene. Kila lililonenwa, likanenwa juu yake.

‘Tamaa ya madaraka,’ wakasema.

‘Mshenzi tu yule, alifikiri ataiweza serikali!’ Wengine wakasikika.

‘Nilijua tu, wasingeweza… mbona miaka ile walishindwa? Wangeweza leo!’ Akina mama nawo hawakuwa mbali katika kuchagiza.

‘Nduli Amin mwenyewe katimua mbiyo, mwaka jana tu hapo, seuze wao’. Maneno chungu mbovu yakamwagika kutoka katika vinywa vya Watanzania. Lakini kubwa kuliko yote, mpaka dakika hiyo, wenye busara wa;lisubiri kusikia japo sauti ya mpendwa wao. Aliyewatoa kwenye makucha ya mkoloni akawaweka huru na kuwafanya watembee wakijigambia Utanzania wao. Kifua mbele, macho mita mia moja. Kimya, hakukusikika lolote redioni. Vipindi vya kila siku vilikuwa vikiendelea. Ilipotimu saa nne asubuhi, pindi tu iliposikika ngoma maarufu ya Hayati Morris Nyunyusa, watu wakajazana redioni. Wasio nazo wakagonga hodi kwa jirani. Habari ni ile ile, kilichoongezeka ni, tu, ‘wengine wanatafutwa’.

‘Wanatuficha, anaweza kuwa ameshauawa, mbona hatumsikii na zaidi wanatuasa tu kuwa watulivu?’ wengine wakadukudukisha mara baada ya dakika kumi za habari kukatika na kufuatiwa na matangazo ya vifo. Maadam serikali iliwataka watu wake kuwa watulivu, walitii.

* * *




IKULU KIKAO CHA DHARULA


Saa tano asubuhi ya siku hiyo hiyo, kikao cha dharula kikafanyika katika ukumbi wa Ikulu. Katika kikao hicho mawaziri wote walikuwepo. Wakuu wa majeshi na vitengo nyeti vya usalama, wote walikutana. Mbele yao, katika meza kuu aliketi Makamu wa Rais na Waziri Mkuu.

“Nchi yetu imeingia tena katika matatizo makubwa. Hii ni aibu kwa taifa!” akaongea kwa mamlaka.

“Leo, majira ya saa kumi na mbili asubuhi, waasi kutoka ndani ya jeshi letu tukufu, wamevamia makazi binafsi ya mzee wetu, Rais wa nchi kwa minajiri ya kufanya mapinduzi,” akasoma katika taarifa aliyoandikiwa. Akatulia kwa sekunde chache na kuendelea.

“Wanajeshi hao waasi walikuwa wakiongozwa komando aliyejulikana kwa jina la Jairos Simbamwene. Nasema aliyejulikana kwa kuwa sasa ni marehemu. Ameuawa na wanausalama wetu watiifu alipokuwa akijariobu kutoroka. Wengine waliouawa ni watatu, na waliobaki wanashikiriwa kwa mahojiano. Ndugu mawaziri, na wakuu wa majeshi, mpaka dakika hii uchunguzi unaendelea na tunahakikisha wote wanaohusika watakamtwa na sharia itachukua mkondo wake,” akakohoa kidogo. Baada ya minong’ono kidogo akaendelea kuwahabarisha.

“Najua, nyote mna hamu ya kujua hatma ya mtukufu Rais wetu. Napenda kuwahakikishia kuwa, waasi hawajamgusa kabisa wala kumwona. Anaendelea vyema, mzima bukheri wa afya na muda si mrefu mtamsikia, ila si leo,” aliposema haya minong’ono ikaongezeka maradufu.

Baada ya hapo, ikafuata taarifa kutoka kwa Waziri wa ulinzi juu mambo yalivyo kiusalama. Majukumu yakapewa kwa idara ya usalama wa taifa. Na kila mtu kadiri ya nafasi yake, akapewa maelekezo ya nini cha kufanya.

Ndani ya chumba hicho cha mkutano, Waziri Kibwana Mtokambali alikuwa kimya akifuatilia kila kilichokuwa kikizungumzwa. Mikono yake alikuwa kaifumbata kifuani, si kama anyehisi baridi, la, bali alikuwa akihisi baridi kali. Watu wakaanza kutawanyika, kwenda kwenye majukumu yake.

Mtokambali aliinuka kitini, hakusalimiana na mtu. Moja kwa moja akaliendea gari lake na kujitoma ndani.

“Nipeleke nyumbani mara moja!” akamwamuru dereva, naye akatekeleza aliloambiwa na mkuu wake. Akili ya Mtokambali ilikuwa mbali kama miisho ya jina lake. Moyo na fikra vilitembea safari isiyojulikana.

Ukichelewa hapa saa sita tu, utakuwa mikononi mwa polisi wenye hasira! Sauti ile ya ndani ikamwambia.

“Nishushe hapa mara moja,” akamwamuru dereva. Naye akaegesha Landrover lile pembeni. Mtyokambali akateremka. “Naingia dukani mara moja, nahitaji kununua dawa za maumivu, sijisikii vyema. Nisubiri, usiondoke…!” akamwambia dereva. Hatua kama ishirini hivi zikamfikisha ndani ya duka lile kama alivyoahidi. Dakika kumi, ishirini, thelathini zikapita. Yule dereva aliendelea kupia miyayo akiwa nyuma ya usukani. Alipochoka, akateremka na kumfuata. Ndani ya duka lile alimkuta mzee wa Kihindi. Alimgundua kutokana na tabani lake kichwani.

“Samahani Kanjbahi…”

“Bila samahani kijana …” yule mzee akamjibu.

“Mhesimiwa Mtokambali ameingia hapa, lakini simwoni kurudi wala kutoka…” yule dereva akaeleza.

“Hujamona! Bona ni muda ile ile yeye toka ije? Mwangalie bizuri nje bhana!” akamjibu na yule dereva akatoka nje kumtafuta mkuu wake. Hayupo.



LISBON – URENO


23 Julai, 2003


Kamanda Amata, alitulia kimya kabisa huku akiwa kaliegemea gari alilokuwa akitumia, Audi TT. Gari hii alipewa maalumu kwa kazi yake aliyotuma kuifanya katika jiji la Lisbon. Halikuwa kubwa, liliweza kubeba watu wanne tu. Pembeni yake alisimama mtu mwingine, mwanamke wa makamo, mvi moja moja kichwani mwake zilidhihirisha hilo. Hakuwa mwingine, Madam S.



Pembeni yake alisimama mtu mwingine, mwanamke wa makamo, mvi moja moja kichwani mwake zilidhihirisha hilo. Hakuwa mwingine, Madam S.

“Usirudie kosa la mwaka jana,” Madam S akamwambia Amata.

“Kosa gani?” akamjibu kwa swali huku macho yake akiwa ameyatupa mbali, akitazama machweo ya jiji hilo.

“Ilitakiwa umhoji kwanza kabla ya kuondoa roho yake…” Madam S akamwambia kijana wake huku akijaribu kuweka vyema kitambaa cha kichwa kilichokuwa kikisukwasukwa na upepo.

“Haikuwa na haja ya kumhoji mjinga yule…” kutokea upande aliokuwa anatazama, akaeuka kule aliko Madam S, “Kwani ulinituma kumuua au kumhoji?” akamuuliza.

“Yote mawili; moja kwenye maandishi na jingine akilini mwako. Tumia common sense wakati mwingine,” akamwambia.

“Jeuri yule, ndo maana nikatimiza andiko kama lilivyoandikwa,” Amata akajibu.

“Sawa, ila tunahitaji vitu kidoo ili kuweka kwenye maktaba yetu,”

“Yeah!”

“Usifanye hivyo safari hii… nipo hapa kwa sababu namhitaji mtu huyo. Ana funguo,” Madam S akamwambia Amata.

“Sawa, zitapatikana. Nitakuletea popote ulipo,” Amata akajibu.

“Vyema!” Madam S akamjibu. Dakika hiyo hiyo gari dogo aina ya Ford Escort likawasili na kusimama mbele yao.

“Tutaonana baadae. Kumbuka kufika Casa De Juncal saa mbili usiku huu, meza namba 5,” Madam akamwambia huku akiingia ndani ya gari lile dogo, lakini la kifahari sana. Akatokomea mjini na kumwacha Amata akiwa pale pale. Kijana huyu nadhifu, mwenye tambo la kuvutia warembo, alibaki pale kwa dazeni za dakika akiwa anasubiri asichokijua. Iza likaingia na kumkuta pale pale akiwa amesimama na kuegemea gari lake. Kama aliyegutushwa, akainua mkonowe na kuangalia saa. Saa moja usiku. Akaingia garini na kuketi kwa utulivu nyuma ya usukani.

* * *


Casa De Juncal


Casa De Juncal ilikuwa umabli wa kilomita sitini kutoka pale alipokuwa Amata kwa muda huo. Ingempasa kuendesha gari kwa muda wa wastani wa saa nzima ili kufika. Muda aliotakiwa kufika, na ule aliopo hapo unemtosha kabisa kufika na kusubiri wakati akipata cappuccino. Akatia injini moto na kuingiza gari barabarani, tayari kwa safari. Avenue de Terra Nova, ndiyo barabara aliyoitumia. Kwa kasi aliyokuwa akienda, isingemchukua saa nzima labda apambane na foleni za barabarani katika jiji hilo. Alipofika njia panda, karibu na magahawa wa Ritiro do Volante, akakunja kulia na kuufuata mzunguko wa Igreja Nova. Akachukua barabara ya kushoto iliyomfikisha katika mgahawa uo baada ya dakika arobaini kupita. Kama angekuwa mwenyeji basi angeweza kupita njia za mkato, lakini haikuwa hivyo.

Kamanda Amata akaegesha gari lake nje ya mgahawa huo. Ukiliona kwa nje jengo hilo, utalidharau, kuukuu, limechoka. Lakini kwa ndani lilikuwa maridadi hasa, lilipambwa likapendeza.

Viti vilipangwa kwa mtindo wa kipekee, upande huu vitatu vitatu kila meza, kule viwili viwili nk.

Amata akaangaza macho na kuitafuta meza na tano hasiione.

“Como você está Senhor! Posso te ajudar?” sauti laini ya mwaDanada mhudumu wa mgahawa huo ikamsabahi na kumuuliza kama anahitaji msaada.

“Sim por favor! Estou procurando uma mesa numbe cinco?” Amata akamjibu kwa Kireno cha kubabaisha, akimtaka aoneshwe meza namba tano.

“Está bem! me siga...” yule binti akamjibu kuwa amfuate. Amata akafanya hivyo. Yule binti mhudumu, akatangulia na Amata akafuata nyuma. Ndipo alipogundua kuwa, binti yule alikuwa amevalia sketi fupi iliyoruhusu robo tatu ya mapaja yake kubaki wazi. Akigeuka kwa mbele huwezi kujua hilo kutokana na apron aliyovaa, iliyofunika vizuri upande huo. Alikuwa mwembaba, mrefu kiasi, alimpita Amata kwa takribani sentimeta tatu. Mwendo wake wa ki-paka ndiyo haswa uliokuwa ukimvuatia kijana huyu.

Upande wa nyuma wa jengo hilo kulikuwa na ghorofa moja ndogo. Sakafu yake ilikuwa na viti vichache sana. Viwili, kila meza. Palikuwa tupu, ni mishumaa tu iliyokuwa ikiwaka katika meza hizo. Moja kwa moja akamwongoza mpaka katika meza hiyo.

Alipokuwa akiketi tu, upande wa mlango akainia mwaDanada mwingine, aliyevalia suti ya kijivu ya gharama. Akavuta hatua mpaka kwenye meza ileile na kuvuta kiti. Akaketi kwa mtindo wa kutazamana na kijana huyo.

“Oh!karibu sana Madam...” yule mhudumu akamkaribisha mwaDanada huyo.

“Asante sana, tuletee Gin Tinto Premium, nyekundu,” yule mwaDanada akaagiza huku jicho lake likiwa limeganda kwa Amata.

“Umejuaje kama nilitaka kinywji hicho?” Amata akauliza.

“Najua. Nilikuwa natembea mawazoni mwako kabla... karibu sana Ureno Kamanda, jisikie upo nyumbani...” akampa mkono, wakasalimiana, “Naitwa Dana...” akajitambulisha.

“Amata Ric!”Amata naye akajitambulisha kwa ufupi sana. Dana akamkazia macho Amata na kumtazama kwa makini. Kisha akajitazama kifuani na kugundua kuwa kifungo cha blauzi yake kimefunuka, hivyo kilifanya matiti yake yaonekane kwa ukubwa kiasi. Naam! Yalikuwa matiti yaliyojaa vema katika sidiria ndogo iliyotosha katika kifua chake. Akakifunga kifungo kile na kujiweka sawa.

“Sicho kilichotukutanisha!” Dana akasema huku sura yake ikiwa imebadilika kabisa.

“Najua! Kilichotukutanisha ni Vincent Mwanachia...” Amata akamwambia.

“Right! Huyu bwana siku nzuri ya kumpata ni kesho,” akaanza kueleza kile kilichowakutanishha.

“Kwa nini isiwe leo?” akamsaili.

“Kesho ndo mambo yatakuwa mukashara... kutakuwa na tafrija ya mikate mikavu katika mgahawa wa Casa de Tostas Absurdo…”

“Mikate mikavu?” Amata akamkatisha.

“Ndiyo, mikate iliyochomwa yaani tosti… ila sasa hii inaokwa mpaka inakuwa kama inaunua vile. Ni tafrija inayokutanisha matajiri tu. Na katika pekua pekua zangu nimegundua kuwa ana mwaliko wa kuwa pale,” akamweleza.

“Ulikuwa na black bag job?” Amata akamuuliza kwa vilugha vyao vya vificho akimaanisha kama ilimpasa kuipekua nyumba au ofisi yake.

“Ilibidi, maana jamaa haonekani ovyo, nilichofanikiwa ni hiyo kadi tu ya mwaliko…” akamwelea Amata ambaye alikuwa akiyarekodi kichwani mwake.

“Hongera sana! Unastahili zawadi,” Amata akamtania. Wakati huo huo kile kinywaji kikawasili, bilauri mbili zikifuatana nacho. Dana akalipia kabisa na yule mhudumu akaondoka eneo lile.

“Tafrija inaanza saa kumi na mbili jioni, kesho. Lakini uwe mwangalifu kwa kuwa jamaa ana yaya wengi,” Dana akamhabarisha Kamanda.

“Cheers!” Amata akamwambia Dana huku akiipuna bilauri yake juu na mwanamke huyo naye akafanya vivyo hivyo, wakagonga na kunywa kidogo kabla ya kuzishusha mezani.

“Casa de Tostas Absurdo!” Amata akarudia kulitaja jina lile.

“Haswaaaa!” Dana naye akamhakikishia kuwa ni hapo hapo.

“Asante kwa maelekezo, nitamnyakuwa kama mwewe afanyavyo kwa vifarana vya kuku…” Amata akamwambia Dana huku bilauri yake ikiwa sentimita moja kutoka kinywani mwake.

“Mi nimemaliza… niruhusu niende,” Dana akaaga.

“Mbona mapema? Hebu kumbuka, yanipasa kukaa mpweke mpaka kesho saa kumi na mbili jioni. Muda huo utapitaje kwangu?” Amata akaanza uchokozi. Dana akaingiza mkono katika blauzi yake, akatoa kimkebe kidogo. Ndani kijimkebe hicho akatoa kadi biashara yake na kumuwekea Amata mezani.

“Nipigie kuanzia saa tano usiku,” akamwambia na kuondoka zake. Kamanda Amata akabaki pale mezani, akiitazama chupa ya Gin Tinto Premium, kazi bora kabisa kutoka Ureno.

Casa de Tostas Absurdo! Akawaza na kuchukua simu mara moja. Akapekua upande waramani na kujaribu kuitazama, walau ajue ni upande upi ilipo. Sekunde hamsini tu zikatosha. Kilichomshangaza ni kuona kuwa mahali alipokuwa amesimama na Madam S ni kilomita tatu tu kufika hapo. Akainua bilauri yake kupiga funda moja, akaishusha mezani. Mara baada ya kuitoa kinywani bilauri ile, akaundua kuwa ana meni mezani pake.

“Wewe ni nani, unajikaribisha pasi na karibu?” Amata akamuuliza. Meni huyo alikuwa mwanamke wa Kizungu. Umri wake tunaweza kuukadiria kati ya miaka thelathini na thelathini na tano hivi.

“Eu sou chamado Quinta!” Akajibu mwanamke yule kuwa anaitwa Quinta.

“Nikusaidie nini, aaanh Quinta?”Amata akamuuliza hukiona wazi kuwa pombe ile inataka kumzidi nguvu.

“Mimi ni mfanya biashara, kahaba, je utapenda kuwa nami usiku huu?” Quita akamuuliza Amata. Hii ilimchukua kama sekunde kumi na tano hivi kuitolea majibu.

“Labda!” akajibu.

“Mwanaume hatakiwi kusema labda. Jibu ndio au hapana,” Quinta akamwambia Amata huku akimtazama kwa macho yake ya bluu. Kope zake ndefu na midomo iliyopakwa rani nyekundu, vilimfanya aonekane kama mtu wa kuchora.

“Labda!” Amata akarudia tena jibu lake na kuona jinsi mwanamke huyo alivyokunja sura kama kaona kinyesi. Akainuka tayari kwa kuondoka. Amata akabaki tu kumtazama asimsemeshe kitu. “Nimeshalipwa pesa kwa ajili yako, tutaonana baadae! Ukitaka kuokoa maisha yangu, lala na mimi...” Quinta akamwambia Amata na kuondoka eneo lile. Kengele za hatari zikalia kichwani mwa Amata, akaelewa nini kinachofuata baada ya hapo.

‘Ukitaka kuokoa maisha yangu, lala na mimi’. Kauli hii ikajirudia kichwani mwa Amata.

Imeshajulikana kuwa nipo? Nani aliyemlipa pesa kwa ajili yangu? Nani kamtishia kumuua? Akajiuliza. Kabla ya kusimama akapia tena funda jingine la Gin Tinto, kisha akasimama na kuondoka zake huku akiiacha ile chupa mezani ikiwa robo.

“Simpendi mtu anayetoa uhai wa mwenzake bila sababu ya msingi,” akajikuta akijisemea huku akishuka ngazi kuelekea chini. Moja kwa moja akaingia katika gari lake na kuketi nyuma ya usukani. Akawasha na kuliondoa eneo lile akaanza safari kuelekea hotelini kwake Epic Sana, Barabara ya Engenheiro Duarte Pacheco 15.

Akiwa tayari katika barabara ya De Casai Lage, akasikia ving’ora vya polisi nyuma yake. Akatazama kwenye kioo na kuona gari la polisi nyuma yake likimwashia taa. Amata akawasha indiketa na kutoa gari nje ya barabara, akasimama.

“Ola somos policiais. Precisamos inspecionar seu carro,” askari mmoja akaja dirishani na kumwambia kuwa wanahitaji kukagua gari lake.

“Ok!” akawaruhusu. Wale askari wakazunguka lile gari na kuomba vibali vyote.

Wakavikagua na kukuta vipo sawa kabisa. “Unajua kwa nini tumekusimamisha?” mmoja akamuuliza.





Ok!” akawaruhusu. Wale askari wakazunguka lile gari na kuomba vibali vyote.

Wakavikagua na kukuta vipo sawa kabisa. “Unajua kwa nini tumekusimamisha?” mmoja akamuuliza.

“Sijui,” Amata akajibu.

“Hili gari limehusika kwenye uhalifu jana alfajiri, na tulikuwa tunalitafuta,” akaeleza askari mmoja.

“Mi sijui, mi nimelikodi jana mchana baada ya kuwasili Lisbon na sikuambiwa kama lina rekodi ya uhalifu...” Amata akajibu.

“Fungua buti!” mwingine akasema. Amata akavuta nobu ndogo chini ya kiti na kuruhusu buti la gari hilo kuachana na loki yake.

“Njoo nje ufungue mwenyewe,” akaamriwa.

Amata akashuka na kuliendea buti upande wa nyuma, akafungua na kujikuta akirudi nyuma hatua tatu. Hakukubaliana na nini anakiona ndani yake. Maiti. Maiti ya mwanamke. Alipotaka kugeuka akajikuta akitazamana na mitutu ya bastola.

“Weka mikono kichwani!” akaambiwa. Amata akatii.

“Piga magoti,” mwingine akaamuru. Amata akatii. Akapiga magoti huku mikono ikiwa kichwani. Akajaribu kuvuta kumbukumbu ya mwili aliouana ndani ya buti lile. Ni wa mwanamke. Mwanamke yule aliyemfuata na kumwambia kuwa amelipwa kwa ajili ya kulala naye.

Nani kamuua? Akajiuliza, hasipate jibu.

“Wahalifu kama ninyi ndiyo tunaowatafuta! Umeua huyu mwanamke jana asubuhi na maiti unazunguka nayo. Sasa utawajua Wareno ni akina nani asee...” askari mmoja akasema huku akiongea na radio call yake. Amata akajiuliza, iweje akutane na mwanamke huyo jioni ya siku hiyo na aambiwe ameuawa jana?

Wamemuua! Akawaza. Akili yake ikaanza kufanya kazi haraka, akagundua kuwa hayupo mikononi mwa polisi bali watu tofauti kabisa. Wamejichanganya. Wakati askari yule akiongea na redio yake, huyu mwingine alikuwa bado kamwekea bastola kichwani. Akampigia hesabu kali za kumfanyia shambulio la ghafla, akifikiria tu atumie sekunde tano kumtyoa uhai.

Amata akashusha mikono yake ghafla, akamkamata mikono yule askari kisha akambinua na kiumbwaga mbele yake. Yule jamaa akatua kama mzigo. Haraka, Amata akainuka na kumuwahi akaukamata mkono wenye bastola na kumlenga yule aliyebaki, akammaliza.huyu mwingine alipojaribu kufurukuta, akamkamata kichwa na kuizungusha shingo, akamvunja na kumuua. Akainuka na kujipukuta vumbi. Akatumia dakika chache kuwapekua marehemu wake. Akachukua kila alichoona kinamfaa na kuvitia mfukoni mwake kisha akacukua ile maiti ya yule mwanamke na kuitia kwenye ari lile walilokuwa wakitumia wale askari. Akaingia garini na kutokomea. Yote hayo yakitukia magari yalikuwa yakipita tu bila kusimama.

Nusu saa baadae aliwasili hotelini kwake. Badala ya kuegesha gari katika maegesho ya hoteli hiyo, akatafuta mahali pengine. Mita mia tano kutoka hoteli ya Epic Sana, kisha yeye akarudi kwa miguu. Ndani ya hoteli hiyo kulikuwa na shughuli nyingi kama kawaida. Akapita kaunta na kuchukua kadi-fungushi. Mbele ya mlango wa chumba chake, ghorofa ya nne, akasimama na kusikiliza kwa umakini kama kuna mtu au chochote ndani. Kimya! Akachanja kadi yake na kufungua mlango. Akaingia kwa tahadhari kubwa, akipepesa macho huku na huku. Hakuna mtu wala kitu cha hatari. Akaingia na kujitupa kitini. Akatoa kila alichochukua kwa wale jamaa. Akavitazama haraka haraka, havina maana, akavitupia mezani na kujiandaa kuingia bafuni kuoga. Tayari alikwishajua kuwa uwepo wake ndani ya jiji la Lisbon umejulikana.

* * *


Upande mwingine wa Lisbon


Nje ya jiji la Lisbon, katika nyumba ndogo, kando ya bahari watu wawili walikutana. Vincent Mwanachia, mwanajeshi aliyeshiriki katika jaribio la kuipindua serikali mwaka 1980 na mwanamama Bi. Jesca Tibatulanwa, mwanaharakati aliyekimbilia Ughaibuni miaka mingi. Wote hawa walikuwa mwiba kwa serikali. Mwanachia alikwishahukumiwa kifo pamoja na wenzake watatu. Mwanamke huyu alipewa vitisho kadha wa kadha na serikali kwa sababu ya msimamo wake. Wawili hawa waliungana na kuwa marafiki sana kwa sababu tu ya itikadi zao. Mwanachia, hakuwahi kurudi Tanzania tangu atoroke mwaka 1980. Arudi afanye nini? Auawe? Dakika chache kabla ya kukutana na mwanamama huyu, alikuwa kwenye mkutano kwa njia ya video yaani video conference. Mkutano ulimkutanisha na wengine walio nchi tofauti, ambao kwa pamoja waliunda Cyndicate yenye sera ya kuiangusha serikali madarakani.

“Bado tunaihitaji ile nchi... watu wachache wameiteka na kuifanya yao!”Mwanachia akamwambia Bi Jesca.

“Tupambane tuikomboe... mimi nina ushawishi mwingi kwa Watanzania, na maadam mmekubali kuniweka kwenye timu hii, ambayo tunania mamoja, tutauwasha moto...” Jesca akamwambia Mwanachie, naye akatikisa kichwa juu chini kukubaliana naye.

“Na wewe lazima upambane, kumbuka serikali imesambaratisha familia yenu. Baba yako amenyongwa kwa kosa kama hili... lazima utimize ndoto ya marehemu baba yako,” Mwanachia akamwambia Jesca.

“Haswaaaa!”

“Lakini sasa kuna jambo linafanyika, mwaka jana aliuawa mwenzetu Titus Mwakibinga kule Brussels...” akasema.

“Ina maana mnawindwa?” Jesca akauliza.

“Siyo m’, sema tu’,” Mwanachia akamrekebisha huku akimmiminia kinywaji kwenye bilauri.

Wakiwa bado bustanini wakibadilishana mawazo, simu ya Mwanachia ikaita kwa fujo. Akaikwapua kutoka katika mfuko wa koti la suti aliyovaa. Akaiweka sikioni mara tu alipobonya kitufe cha kuruhusu simu hiyo izungumze.

“Yes...” akaitikia namna hiyo huku akisogea kando kusikiliza ujumbe anaofikishiwa. Kutoka mbali, Jesca alimuona mzee huyo akibadilika sura, akienda huku na huko. Mara akatulia, akakata simu na kuirudisha mfukoni, kisha akavuta hatua mpaka kwa mwanamke yule.

“Tuondoke!” akamwambia. Bila kubisha wala kuuliza, Bi. Jesca akainuka na vijana wanaomloinda mzee huyo wakawafuata nyuma mpaka kwenye gari lake.

“Nini kimetokea?” Jesca akauliza wakati gari lile likiondoka taratibu.

“Bastard!” Badala ya kujibu, akatukana.

“Kuna mwendawazimu ameingia Lisbon!” akaoneza kusema huku akitoa kitambaa chake na kujifuta jasho asilokuwa nalo.

“Kuna mtu katumwa kutoka nyumbani, kuja kiniua...” Mwanachia akamwambia Jesca.

“Nyumbani?”

“Ndiyo! Yaani Tanzania. Mwaka jana mwenzetu mmoja aliuawa Brussels. Tukafanya utaratibu wote ili kumjua, tukafanikiwa. Tukapanga watu ili kujua nyendo zake. Tukapata taarifa kuwa anakuja Lisbon, nikiwa na maana ananifuata mimi ili atimize alilotumwa...”

“...akuue?” Jesca akamkatisha kwa swali.

“Ndiyo. Sasa kuna mtego tulimtegea, ameutegua na ameua vijana wetu wawili ambao tunawatumia sana kwenye genge letu... dah! Mshenzi huyu nitahakikisha kesho haioni,” Mwanachia akajibu na kuongeza maelezo ya ziada. Kutoka ndani ya lile gari, Mwanachia alitoa taarifa kwa wenzi wake juu ya tukio hilo.

* * *

Mara baada ya kuuawa Titus Mwakibinga kule Brussels, Ubelgiji, iliwawia ugumu mkubwa sana TSA kutambua wapi walengwa wengine walipo. Wote wanaounda sindiket hiyo walitoweka ghafla baada kifo kile kwa kuwa walijisahau na kudhani kuwa wamesahaulika.

ITAENDELEA

2 comments:

BLOG