Search This Blog

Saturday, February 26, 2022

SEKESEKE (ROHO MKONONI) - 3

   

Simulizi : Sekeseke (Roho Mkononi) 

Sehemu Ya Tatu (3)





Inspekta wa jeshi la polisi John Butu anapokea barua ya kuamishwa kazi,jambo hilo anapingana nalo na kuamua kuandika barua ya kuacha kazi kabisa je unadhani nini kitaendelea?!


Tusonge katika hatua nyingine kuendelea kuburudika zaidi


HATUA YA KUMI NA MOJA:


Tayari akili yake ilishagubikwa na ukungu wa kukurupuka,


Akupenda hata kuchukua wasaa angalau dakika moja na ushee aidha kutafakari kile akifanyacho.


Tabia hii kila mara ndo ilo mfanya ajutie kile aamuacho kwanzia kumuua yule mwandishi,kumuua huyu alo mjua kama mr x na pia kuandika barua ya kuacha kazi,akaikabidhi kwa bosi wake,akuishia hapo akapiga

saluti muinuko,na kutoa kofia yake ya polisi akaiweka mezani,palepale akageuka na kuuendea mlango,hata mkuu wake alipo muita akuangaika kugeuka,alisha amua,na Butu kawaida yake akiamua kaamua huwa arudi nyuma.


Askari wenzake walishtuka kumuona katika hali ile,kengele ya hatari ikagonga katika vichwa vyao,ila hakuwa na muda wa kuwaeleza kilichotokea,akaingia ndani ya gari yake kuelekea kwake


Huku nyuma kamishna Nurdin alishika simu yake akapiga namba kadhaa akaweka simu masikioni simu ikaita...


"alooh!"


Upande wa pili ukapokea.


"Mkuu ni kwamba Butu kaacha kazi baada ya kumpa barua ya uamisho!"


"Ushawatangazia wenzake juu ya jambo hilo?!"


"Hapana mkuu!"


"Vizuri na usiwatangazie,haraka sana na kuitaji ofisini kwangu tujadili hili!"


"Sawa mkuu"


Palepale simu ikakatwa,


Pasina kupoteza muda kamishna akajinyanyua na kuelekea nje,ambapo aliingia ndani ya gari yake tayari kuelekea alipopajua yeye.


***


Katika jumba moja la kifahari,maeneo ya Tmk Vetenary,eneo aliloishi Inspekta Butu ilisimama pikipiki akashuka mtu ambapo baada ya kutoa element akavaa kofia la sweta lake lililo muwezesha kuficha sura yake akaanza kuliendea geti la nyumba ile alipofika akaingiza mkono wake ulovalishwa gloves katika mfuko wake wa jeans akatoka na funguo aina ya orlando akaziingiza katika kitasa cha geti akafungua haraka akazama ndani!


Alipofika mlango wa ndani akafanya vivyo hivyo,


Safari yake ikaanzia sebuleni alipopanda juu ya meza ya kioo,akuogopa kuivunja,akategesha kitu juu pembeni ya taa,kitu icho kidogo mfano wa kifungo ilikuwa ni ngumu kuonekana kwa urahisi!.


Alipomalika alishuka na kuelekea upeuni palikuwa pembeni kidogo na eneo lile la kupumzikia,eneo hili la kulia,akapanda juu ya meza kubwa ya mbao,pembeni ya taa akategesha kile kitu chake,sasa akashuka na kuelekea vyumbani,alifanya ivyo ivyo katika kila chumba pamoja na bafuni,sasa akarejea sebuleni peyuni,juu ya meza palikuwa na kompyuta mpakato alimaharufu kama laptop,akaiwasha, katika soketi,ikawaka sasa ikaitaji namba za siri,mtu yule akatabasamu akatoa flash na kuchomeka, akabonyeza bonyeza ajuavyo yeye laptop ile ikafunguka,akaanza kufanya alojua yeye,wakati akiendelea katu akujua nje mwenye nyumba aliwasili.


Alishtuka kukuta pikipiki nje ya nyumba yake,haraka akashuka na kuchomoa pistol yake,kwa mwendo wa haraka tena kwa uangalifu akaanza kunyata kulifata geti akafungua taratibu na kuzama ndani!,akaanza sasa kusonga mbele mpaka kwenye mlango wa nyumba ya ndani,akashika kitasa na kukikunja taratibu ghafla akaufungua na kuzama ndani!


Ile anaingia akapokewa na teke,kwa kuwa lilikuwa ni la ghafla lilimtupa pembeni pistol nayo ikamponyoka,


Mtu yule kwa haraka akauwai mlango na kutoka,


Butu akukubali kumuacha akainuka akaifata bastola yake akaiokota na kuuwai mlango akaufungua na kutoka nje,akaanza kurusha risasi ila mtu yule alikimbia kwa mwendo wa zig zag mpaka kulifikia geti,Butu bado alimmiminia risasi zilizo mkosa kosa,mtu yuld akafanikiwa kufungua mlango wa geti lile akaiendea pikipiki yake akavaa element na kuiondoa kwa kasi,Butu naye akukubali alipofika nje akapanda gari yake naye kuanza kuifukuzia ile pikipiki!.


Mfukuzano uliendelea ila mtu yule alikuja kumpotea makutano ya tazara,akumwona tena hata alipofika buguruni na kujaribu kuuliza akupata ushirikiano mwisho akaamua kurejea kwake,huku kichwani akiwa na mawazo mengi,je mtu yule ni nani!, ndo Mr x au mfuasi wake?,alikuwa anafanyaje kwenye kompyuta yake,aliwaza sana,kichwa kilimuuma kwa mawazo,alipofika kwake akaiendea kompyuta yake na kuifungua,akukuta cha zaidi,akaangaza angaza macho kule ndani pia akuona cha tofauti,akaiendea friji akatoa chupa kadhaa za bia akaweka mezani akachukua glasi na kuanza kuzigida,wakati akiendelea kunywa ghafla akapata wazo,haraka akajinyanyua na kuiendea pikipiki yake,akapanda na kuiondoa,safari yake iliishia katika duka liuzalo kamera za cctv,wakafanya maongezi akalipia,mafundi wakaingia kwenye gari yeye akaongoza mbele na pikipiki yake safari ya kuelekea kwake ikafatia,aliamua kwenda kufunga kamera za ulinzi!...




Inspkta John Butu ana amua kuacha kazi,ni baada ya kupewa barua ya uamisho,


Anarejea nyumbani,ila anashtuka kuikuta pikipiki nje ya nyumba yake kuingia anamkuta mtu akichezea kompyuta yake,mtu yule asiyemfahamu anafanikiwa kumponyoka,Butu anaamua kwenda katika duka la kamera anachukua mafundi na kuwaleta nyumbani wana anza kutegesha kamera za ulinzi katika jumba lile tusonge kujua kilichoendelea...


HATUA YA KUMI NA MBILI


Watu wale wa cctv kamera walifanya kazi haraka haraka,wakiweka nje kwenye mlango kamera mbili sebuleni wakaweka ukutani na katika kila chumba,wakaunganisha na kompyuta zoezi lote likakamilika,awakuweza kuzitambua kamera zilizokuwa ndani ya kidude cha taa juu ya paa la nyumba ile


'Kazi sasa ishakamilika,boya yeyote atakayeingia humu nitamuona tu!'


Butu akawaza.


***


Upande mwingine zilipo ofisi za mkuu wa polisi 'igp' ili ingia gari,maeneo ya maegesho akashuka kamishna Nurdin,akaanza kupiga hatua kuelekea lilipo jengo la ofisi ya mkuu wake yule,njiani alipigiwa saluti.


"Mkuu yupo?!"


Alimuuliza katibu muhtasi wa mkuu wa polisi ambaye alitingisha kichwa kuafiki!


"Kasema ukija nikuruhusu ukamuone karibu kamishna".


Nurdin akujibu kitu akageuka na kuelekea upande ulipo mlango ambao juu kulikuwa na maandishi inspekta jenerali wa polisi 'I G P' alipofika akagonga,akashika kitasa akakizungusha na ku usukuma kidogo kwa ndani mlango akapata upenyo,akaingia,akaurudishia mlango kama alivyoukuta.


Alimpigia saluti mkuu wake,akampa ishara aketi Nurdin akamtwii!


"Lete habari,kijana kakataa uamisho?!"


Mkuu wa polisi alotambulika kwa jina la IGP STEVE jina lake kamili ni Julius Steven akauliza,kabla Butu ajajibu mlango ukafunguliwa na binti ambaye ni katibu muhtas wa Steve


Akaruhusiwa akaingia...


"Mkuu nikuletee nini?,chai,maziwa?!"


"Mletee Arabic ni mpenzi sana wa kahawa huyu jamaa,"


"Na kashata bila kusahau!".


Kamishna Nurdin akadakia wote wakaachia kicheko,


"Na wewe mkuu?!"


Binti akamgeukia bosi wake akamuhoji akimtupia tabasamu mwanana....


"Mi maziwa na bajia"


"Bajia,bagia?!"


Binti akamsahihisha...


"Ivyo hivyo ujuavyo binti!"


Igp akajibu kwa tabasamu binti yule

mrembo akageuka tayari kwa kuondoka.


Akapiga hatua kuufata mlango huku nyuma akisindikizwa na macho ya maafisa wale.


Baada ya kutoka ndipo maongezi yao yaliposhika hatamu.


"Yah,kijana kaacha kazi,kasema kuliko ahame Dar bora aache kazi bado anahitaji kulipiza kisasi!"


IGP akatingisha kichwa kwa masikitiko!


"Na vipi kuhusu upelelezi wa kesi yake?,ulo mkabidhi faili anasemaje?!"


"Amna chochote mkuu kesi ile ni ngumu tena inaonekana hao majamaa wana mtandao mkubwa sanaa"


"Kivipi iwe ngumu na mara ya mwisho ulinambia huyo 0759427653 mlimtia nguvuni?!"


"Mkuu nasikitika kukwambia yule mtu alikuwa siyo na Butu alimuua kimakosa hawa majamaa waliunganisha tu namba,"


"Unataka kunambia yule mlomkamata alikuwa ahusiki kwa chochote?"


Kabla CP Nurdin ajajibu mlango ukafunguliwa na binti yule akaingia mkononi akiwa na visahani viwili kimoja kikiwa na kashata kingine bagia,kashata akakiweka karibu na Nurdin kile cha bagia akakiweka karibu na Steve kisha akatoka.


Nurdin akaendelea....


"Yule mtu alikuwa ahusiki kwa chochote mkuu ni kosa tu lilitendeka na Butu ajui kama mimi najua hili!"


Igp Steve akashusha pumzi nzito,akakuna kichwa chake...


"Sasa nani atakuwa anahusika kwa haya yote?!"


Akamtupia swali,ikawa sasa zamu ya Nurdin kutafakari,kimya kikatanda baina yao,wakati kila mtu akiwaza lake mlango ukafunguliwa yule binti akaingia mkononi akiwa na vikombe viwili vya udongo,kimoja kikiwa na kahawa,kingine kikiwa kimejaa maziwa akaenda kuwaekea,


"Asante Muni kaendelee na kazi"


Igp akamshukuru mfanyakaz wake,


"Huyu kijana anapitia katika wakati mgumu sana,namuonea huruma kwa sasa tumuache afanye anachotaka zoezi zima likimalizika ndipo tumrejeshe kazini!"


Igp akatoa wazo lake,


"Sawa mkuu nitafanya ivyo,"


"Kingine mwambie huyo anayeisimamia kesi yake kila atakachogundua asisite kumwambia,mpaka hao washenzi walio iteketeza familia ya chombo cha dola waipate posho yao,iliniuma sana"


Hatimaye Igp alitoa ruksa kwa Butu kuendelea na kazi akiwa nje ya jeshi,japo Butu akutakiwa kuwambiwa chochote.


Ni wazi jeshi zima la polisi liliumizwa kwa alichofanyiwa.


***


SURA YA TATU


TEMEKE MIKOROSHINI


KATIKA JUMBA MOJA LA KIFAHARI


Katika chumba kimoja ndani walikwepo watu wa tatu,mwanamke mmoja ambaye anaweza fikia umri wa miaka 37 na wanaye wawili mmoja wa kike akiwa kama na miaka 17 huyu alionekana ndo mkubwa na wa pili wa kiume huyu miaka yake kumi na mbili,wote walikuwa katika hali ya majonzi,humo ndani walipokwepo hawakuwa huru!.


Walifungiwa!.


Chakula waliletewa na watu walojifunga nyuso zao,kutoruhusu sura zao zionekane,kuoga walioga humo humo,walitekwa na awakujua walitekewa nini,awakuambiwa chochote,siku ya tatu sasa ilishapita toka kutekwa kwao!


Awakujua wapo wapi kwani waliletwa wakiwa wamefungwa macho na walipofunguliwa wakajikuta katika chumba kile,hawakupewa mateso yoyote!...


Siku hii kama kawaida mlango ulifunguliwa,wakaingia watu wa tatu wote wakiwa wamefunika nyuso zao,ilikuwa ni mapande ya usiku!...


Kama saa moja na nusu hivi


"Leo mnarudi kwenu!"


Mmoja kati ya watekaji wale alizungumza,akawapa ishara wenzake wakawafunga vitambaa katika nyuso zao,wakawaswaga mpaka nje wakawaingiza kwenye gari safari ya kutoka katika jumba lile ikafatia...


Gari ile ilienda mwendo mfupi kabla ijaingia lami na kuchukua uelekeo wa tazara maghorofani,ikaelekea mpaka buguruni,safari yake ikaishia Tabata Matumbi ikaingia katika barabara ya vumbi na kuacha lami,ikakatiza mitaa kadhaa na mwisho ikasimama katika nyumba moja nzuri ya kifahari pia,watu wale wakafunguliwa vitamba usoni mwao,hawakuamini!,ni kweli mbele wali iyona nyumba yao,


"Mama tumewa achia huru atujawatesa wala kuwa ekea alama yoyote,usiripoti polisi kwa chochote juu ya utekaji huu na wala msiende polisi kuripoti chochote kama mnapenda kuendelea kuishi! Sawa?!"


Dereva akamta adharisha mama,alotingisha kichwa kukubali!


"Mkienda kinyume na ichi tulichowaomba tutawachukua na Safari hii amtaishi Kama mlivyoishi hapo awali nadhani mmenielewa"


"Sawa baba tumekuelewa atutaripoti chochote"


Mama yule akajibu kwa unyenyekevu


Dereva akampa ishara kijana mmoja akafungua mlango mama na wanaye wakashuka na gari ile ikaondoka,wali isindikiza kwa macho mpaka ilipoishia ndipo walipopiga hatua kuifata nyumba yao!.


Pamoja na yote wakati ile gari inaondoka mama yule alifanikiwa kuzikaririsha namba za gari lile.


Furaha sasa ilitanda ndani ya mioyo yao,wakalifikia geti na kubonyeza kengele wakasubiri wafunguliwe,geti lilionekana kufungwa kwa ndani!.


No 13&14


Ni katika mazingira ya kutatanisha familia moja ilitekwa,mama na wanaye wawili,wa kike na mdogo wake wa kiume,walikaa kwa muda wa siku tatu wakaachiwa tena wakapelekwa mpaka kwao,wakafunguliwa vitambaa usoni kabla ya kushuka dereva alimuonya mama yule kutoripoti chochote polisi,mama yule alikubali,ila alikaririsha namba za gari lile,je ni watu gani wale,kwa nini walitekwa na walitekwa na watu gani?! Tusonge


*HATUA YA KUMI NA TATU NA YA KUMI NA NNE*:


Walisubiri kwa muda punde hatua za mtu akikimbia kwa ndani zikasikika,


Na ghafla ikasikika kuguswa kwa geti kama kufunguliwa kwa komeo lililopo ndani,geti likafunguliwa.


"Heeee mamaa!"


Akatoka binti mrembo akamkumbatia yule mama kwa furaha!.


"Salima mwanangu nilishakwambia kabla ujafungua geti uwe una uliza kwanza ni nani?!,we unakimbilia kufungua geti je angekuwa mtu mbaya?"


Mama alianza kuteremsha lawama baada ya kumwachia m

yule binti alotoka ndani ya ile nyumba sasa wakawa wakiingia ndani


"Sawa mama nimesikia,mlienda wapi nawapigia ampatikani mjini ikawa mjini kweli!"


Wakati wakiingia ndani yule binti akaendeleza stori


"Yani we acha,kwanza baba yako yupo?!"


Mama akajibu sambamba na kumpachika swali binti yule.


"Hayupo! toka ile siku mlo ondoka ajarudi nikajua mko wote! "


"Eti?!, Unasema?!"


Mama yule akahoji kwa mshangao pasina kuamini kile alichokisikia.


"Baba ajarudi toka juzi mama,na watu wengi wamekuja kumuulizia wengine wakiwa wafanyakazi wenzake"


"Jamani mume wangu atakuwa salama kweli?!"


Mama aliuliza huku machozi yakimmwagika,walifika sebuleni mama akatangulia kuweka simu yake chaji,ilishazima toka ile ile siku ya kwanza walipotekwa.


"Ukwenda polisi kutoa taharifa juu ya upoteaji wetu?!"


Mama akazidi kumdadisi yule binti...


"Sikwenda mama,mi nilijua mtarudi!"


"Hapana Salima,hali kama hii siku nyingine ikitokea katoe taarifa kituo cha polisi kikawaida atuwezi kusafiri bila kukuaga,ungekaa utusubiri mpaka lini tungekufa je?!"


"Kwani ni nini kilichotokea mama?!"


Ikabidi sasa yule mama aanze kumsimulia mfanyakazi wake kilichowapata!...


"Siku ile nilipokea sms kutoka kwa mume wangu,sms hiyo ilisema kuna gari itakuja kutuchukua hivyo nijiandae basi nikamwambia Martha na Bray wajiandae kweli gari iliwasili tukatoka na kuingia,ile tumeshakaa vioo vikapandishwa palepale tukawekewa silaha tukafungwa macho atukujua tulipopelekwa,tulikuja kuambiwa tushuke tukapelekwa tulipofunguliwa vitamba tulikuwa ndani ya chumba,ndipo tulipokaa uko,chakula tuliletewa huko huko,kila kitu tulifanyia humo humo"


"Mh! Poleni kumbe mlitekwa mama?!"


"Ndio na nahisi pengine watu wale walihitaji ela kwa mume wangu ,ila kitendo cha kunambia naye toka juzi ajaja kinanitia shaka sana"


"Baba atakuwa kwenye matatizo mama lazima ukaripoti polisi!"


Brayson mtoto wa wakiume wa yule mama akashauri,kabla dada yake ajadakia


"Hapana mama!,unakumbuka yule dereva alivyosema?!,ukienda polisi watatuua"


Sasa kila mtu akawa akisema lake kwa kuwa simu ilishapata chaji kidogo mama akaifata na kutafuta namba za mumewe akazipiga!,lakini azikupatikana.


Kwao huu ukawa mtihani mwingine, maskini mama akujua kama kwa sasa yeye ni mjane mumewe alishakufa tena kwa kupitia mikono ya aliyekuwa inspekta wa jeshi la polisi John Butu


Ni baada ya kumuhisi mtu yule kwamba ndo 'MR X' ilikuwa hivi!....


SURA YA NNE


UPANDE WA PILI WA SHILINGI


IKULU


Kilifanyika kikao cha siri katika chumba kimoja cha mikutano ndani ya Ikulu ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Ndani walikwepo watu wa tatu,walionekana kuzama katika maongezi yao yalokuwa nyeti


"Mheshimiwa mtukufu Raisi nimemgundua msaliti atoaye siri zetu ni mr Silvester huyu ndiye alimpigia simu afisa wa polisi kwa kutumia namba za siri 15551 na kumjulisha juu ya ule mzigo wetu na pia akamjulisha juu ya mbinu za uokoaji tulizopanga kuzitumia..."


"Saadash Zidu kazi nzuri na nijijua ndani ya masaa 6 utakijua kirusi kilichopo katikati yetu,msaliti wetu utamjua,chakufanya ahukumiwe kifo mara moja!"


Mheshimiwa Raisi akajibu kwa furaha kwani alishajiuliza sana ni nani aliyekuwa na udhubutu wa kuunguza ishu yake polisi mpaka kukamatwa kwa vijana wake na alijua lazima atakuwa mtu wake wa karibu na sasa alishamjua.


"Na si mimi nitakaye muhukumu lah!"


Akashtushwa na kauli ya kijana wake yule alomuamini zaidi ya kitu chochote!


"Bali?!"


Waziri mkuu naye akahoji,Zidu akacheka kabla ajajibu swali lile


"Huyo huyu ampaye habari zetu ndiyo atakayemwangamiza tena kikatili sana"


"Kivipi sasa?!"


Kwa shahuku Raisi Bisau akahoji Zidu akaachia tabasamu tena ,


"Nahitaji niwaoneshe kwa vitendo!"


Alijibu huku akiwa katika tabasamu jepesi,akashika simu yake na kupiga namba kadhaa,akaweka sikioni akasubiri kwa sekunde kadhaa simu ikapokelewa...


"Mzee tunakikao cha siri na muheshimiwa Rais,pamoja na waziri mkuu ivyo tunakuomba nawe ufike hapa katika chimbo langu huku matumbi"


Kumbe kijana yule alikuwa akiongea na Raisi Patrtick Bisau pamoja na waziri mkuu Benson Sai,Zidu alikuwa ni mkuu wa usalama wa taifa ndo mmiliki wa ile namba 0759427653 aliyo iunganisha toka kwenye simu ya Kijana alotambulika kwa jina la Zuberi,na mzigo ule ulikuwa ni wa Raisi pamoja na waziri mkuu wake,ila uliratibiwa na Zidu mwenyewe,Silvestar yeye alikuwa mfanyakazi ofisi ya Raisi akupendezwa na kazi ile kwa siri sana akatafuta namba za siri na kumjulisha inspekta Butu kabla ya kugunduliwa!


Baada ya kumaliza kuongea na mtu yule sasa Zidu akawaomba wakuu wale wa nchi waelekee kwake wakamsubiri huyo kijana


Pasina msafara watatu wale wakaingia ndani ya gari Zidu akiwa dereva Safari ya kuelekea Tabata Matumbi ikafatia.


Dakika kumi tu waliwasili wakawa aKimsubiri Silvester tena kwa hamu kubwa sana.


Pasina kujua alichoitiwa Mr Silvester aliwasili katika jumba ilo la siri la Zidu,akatoa heshima kwa viongozi wale wa nchi akaambiwa aketi!,bila wasiwasi akaketi,Zidu akamuomba simu yake Sili pasina kujua akampa,


"Namba za mke wako umezisevuje huku?!"


Zidu akahoji kishari sasa sura ilibadilika,Sili akajua hapa si salama tena!


"Kuna nini wakuu?!"


Silvestar akahoji kwa wasiwasi!


"Utajua,wewe si msaliti sasa dawa yako ndogo,sema namba ya mkeo umesevuje humu?!"


"Wi..fe" Mzee wa watu akajibu kwa woga huku akishindwa kujizuia kutetemeka!.


"ha ha ha eti wife,sawa hii hapa!..nimeiona"


Zidu akatuma meseji aloijua yeye,kisha akaifuta na kumrejeshea mwenyewe simu yake,muda ule ule akatoa simu yake na kuwapigia watu wake...


"alooh,Isack naomba muelekee nyumbani kwa Silvestar mke wake na watoto watatoka muwapandishe kwenye gari muwafunge macho wasijue mnapowaleta muwalete huku matumbi katika nyumba yangu ya siri sawa?"


Upande wa pili ukaitikia sawa,kweli baada ya kama nusu saa gari ile iliwasili,wakiwa katika chumba kingine kupitia dirishani Silvestar aliona familia yake ikishushwa na kuingizwa katika chumba kingine!


"Ili kuikomboa familia yako lazima wewe ujifanye mimi!,mimi nitawasiliana na huyo mpumbavu wako na kuhitaji kuonana naye then wewe utaenda kama mimi,utapokea malipo yako ya usaliti kwetu ndipo tutaiachia familia yako ukienda kinyume na hichi wewe na familia yako yote tutaiteketeza katika visima vya mamba,hata mifupa yenu aitoonekana"


Hapo ndipo Mh Rais na waziri mkuu wake waliuelewa ukatili wa Zidu k,hapo ndipo walipo muelewa vizur zaidi,palepale Zidu akatoa simu na kumpigia Butu akahitaji aonane naye kivulini bar usiku wa siku hiyo,


Akawaita vijana wake kadhaa na kuwapa kazi wampeleke hapo bar usiku,na ndivyo ilivyokuwa Sili aliamua kufa kuitetea familia yake,usiku aliingizwa garini mpaka Kivulini walipofika dereva akampigia simu Zidu kumtaharifu kuwa amefika,Zidu akaomba wawili wamsindikize mpaka atakapoketi ndipo waondoke,ikawa ivyo,Silvestar akakamatwa Butu akimjua ndiye mr x wake! na kwenda kumwangamiza kikatili pasina kujua.


Sasa ndo wakaiachia familia yake.


Walipofika nyumbani wakakuta hali ya sintofahamu kutoka kwa binti wa kazi Salima.




Zidu anafanikiwa kumgundua mheshimiwa Silvestar kuwa ndiye aliyempa taharifa afisa wa jeshi la polisi John Butu na kumwezesha kukamatwa kwa unga wa madawa ya kulevya,haraka kikao kinafanyika ikulu na mwisho muheshimiwa Raisi Bisau anatoa amri Silivestar kuuwawa,Zidu anahaidi kumtumia huyo huyo Butu kufanya kazi hiyo na ili linatendeka baada ya kuiteka familia yake na kumwambia ili aiachie huru lazima akajikamatishe kwa Butu kama yeye Silivestar anakubali ili kuikomboa familia yake,je nini kitaendelea?! Tusonge katika hatua inayofuata:


HATUA YA KUMI NA TANO:


Usiku ule hakukuwa na aliye kuwa na hamu ya kwenda kulala,mpaka inatimia saa nane wote walikuwa macho,sebuleni pale wakijadili kipi cha kufanya,japo waliwasha tv ila hakukuwa na aliyefatilia kilichokuwa kikiendelea katika runinga ile,woga uliwatawala!


Bi Glory kwa vyovyote vile alijua lazima mumewe atakuwa kwenye hatari,kama si kupoteza maisha.


Bray alimsisitizia mama yake pakipambazuka aende kituoni,akaripoti,tena kituo kikuu cha polisi,japo Martha alimpinga mdogo wake akisisitiza onyo walopewa na yule dereva,ila bi Glory akakata shauri itakavyokuwa na iwe,atawezaje kukaa kimya bila kwenda kuripoti kupotea kwa mume wake?,na alijua fika akienda polisi pia ni lazima aeleze ukweli,kwamba nao pia walitekwa...


Akazima tv na kuwataka watoto wake wakalale,naye akaelekea chumbani kwake kulala


Kwa kuwa walichelewa kulala pia walichelewa kuamka,Bi Glory kabla ajafanya chochote akachukua simu yake na kumpigia shemeji yake,yani mdogo wake na mume wake,ndo ndugu pekee alokuwa amebakia kwa upande wa mume wake,akamuomba afike nyumbani,kwa kuwa hakuishi mbali kweli alifika akamuelezea,shemeji yake alotambulika kwa jina la Michael alimpa pole sana shem wake!,akamtoa khofu na kumwambia lazima waende kituo cha polisi...


Asubuh ile ile safari ya kuelekea kituoni ikafatia.


***


KITUO KIKUU CHA POLISI


Kamishna Nurdini alikuwa kakaa ndani ya ofisi yake kakasirika,kila dakika aliguna,mdomo aliukunja,si muda mrefu alikuwa ametoka kumgombeza kijana wake Inspekta Jonathan,ni muda mrefu sasa toka amemkabidhi kesi ya afande Butu aloipoteza familia yake,ila mpaka muda ule alotoka kuongea naye kijana yule hakuweza kugundua kitu chochote juu ya kesi hiyo.


Kwa upande wa Jonathan alitoka akiwa na hasira ofisini kwa mkuu wake.


Alikumbuka wao wa nne yani yeye Butu,paul na Andrea walishamuua alosemekana ndo mmiliki wa ule mzigo,walimteka kivulini Bar usiku ule wa kampeleka katikati ya msitu na kumuua kikatili sana!


Cha ajabu baadaye Butu akaja kumwambia mtu yule siye,bali ni yule alokuwa akiwasiliana naye kwa namba 15551 na kumpa maelezo,mpaka muda ule akujua mtu yule ni kwa nini aliamua kuuvaa uhusika wa adui yao na kukubali kufa siri yake ikibaki moyoni,aliwaita wenzake Paul na Andrea ofisini kwake na kuwa ambia jinsi mkuu alivyotoka kumgombeza!


"Unadhani tutafanyaje afande na yule mtu atumjui bora tungeijua hata familia yake..."


Ni wakati wakiendelea kujadili upande wa mapokezi akiwa binti Fatma waliwasili,bi Glory na shemeji yake,walikaribishwa wakaketi Fatma aka anza kuandika maelezo yao!


"Ok! Naweza kuwasikiliza!"


"Eleza kila kitu shem usifiche kitu hapa ni usalama wa raia ivyo toa wasiwasi"


"Ni kwamba siku tatu zilizopita nilitumiwa meseji na mume wangu alinambia nijiandae mimi na wanangu kuna gari inakuja kutuchukua,nikijua ni sapraiz nika wa andaa wanangu punde nikasikia honi nje nikamuaga mfanyakazi nasi tukatoka nje tulikuta gari tukafunguliwa mlango tukaingia,ile tumeingia vioo vyote vikapandishwa juu wale watu wakatubadilikia na kutufunga usoni,sijui walitupeleka wapi,ila tulikuja funguliwa macho tukajikuta ndani ya chumba kimoja,tuliletewa chakula mule,tulikaa siku tatu mpaka jana tulipoambiwa tupo huru tukafungwa macho na kurejeshwa nyumbani ambapo watu wale walitupa onyo kuripoti polisi ila tulipofika ndani na muulza Salima habar za mume wangu akanijibu toka tuondoke naye ajarudi,tukimpigia apatikani sijui mume wangu atakuwa kapatwa na nini!..."


"Salima ndo huyo mfanyakazi wako?!"


Fatma akahoji,


"Ndiyo!"


"Watu hao walowateka walishawapiga,au kukupigeni picha au hata kuwapa simu muongee na mume wako?!"


"Hapana awajawahi!"


"Mumeo anaitwa nani?!"


"Silvestar Emanuely!"


"Anafanya kazi gani?!"


"Yupo ofisi ya Raisi ikulu pale"


"Je ulishawahi kumsikia mumeo akigombana na mtu? au unamjua adui yeyote wa mumeo unaye dhani anahusika katika utekaji wenu,au kupotea kwake?!"


"Hapana afande,"


"Ok,nahitaji picha yake,"


Bi Glory akaingiza mkono kwenye pochi yake akatoa picha ya mume wake na kumkabidhi afande yule,


Fatma alizicheki kwa muda kisha akasimama...


"Naomba mnisubiri..."


Akalinyanyua lile kalabrasha aliloliandika,akapanda nalo juu mpaka katika ofisi ya kamishna,katibu muhtas akamruhusu Fatma akagonga na kuzama ndani!


Alimkuta kamishna bado kanuna,akampa lile faili,kamishna akaanza kulisoma...


"Mh!," Nurdin akaachia mguno akishangazwa na maelezo yale,hakika maelezo yale hayakuwa ya kawaida hata chembe!...





Bi Glory ana amua kwenda polisi kushtaki kupotea kwa mume wake,pia anaelezea juu ya kutekwa kwao,yeye na watoto wake wawili Bray na Martha,walimkuta mapokezi afande wa kike alotambulika kama afande Fatma,afande yule alokuwa na cheo cha u koplo,aliandika maelezo yao kisha akaelekea na faili ofisini kwa mkuu wake Kamishna Nurdin,

Kamishna alipitia yale maelezo mwisho akaguna,je unadhani nini kiliendelea?! Twende katika hatua inayofuta...


HATUA YA KUMI NA SITA


"Hii kesi na mashaka nayo embu kwanza niitie Insp Jonathan hapa..."


"Sawa afande!"


Fatma akatoka na kuelekea ilipo ofisi ya Jonathan...


Kwa upande wa Jona baada ya kumaliza maongezi na wale marafiki zake,ambapo walikubaliana jioni wakutane kivulini bar sambamba na inspekta Butu waongelee swala ilo Jona akawaruhusu Paul na Andrea wakaendelee na kazi!


Wakati wakiwa kwenye korido ndefu wakielekea mapokezi,njiani walikutana na Fatma ambaye yeye alikuwa akielekea ofisini kwa Jona.


"Afande Jona yupo ofisini kwake?!"


Wakati wakipishana Fatma akawapachika swali ambapo wote kwa pamoja walimwitika,Fatma akazidi kukaza mwendo kuifata ofisi ya Jona!


Afande Paul na mwenzake waliwasili mapokezi walisalimiana vizuri na yule mama na wanaye,wakaachana nao,kila mtu akachukua siti yake!,walijua tayari mama yule atakuwa tayari kashasikilizwa,


Jonathan na Fatma waliwasili ndani ya ofisi ya kamishna,wakapewa ishara waketi.


"Nimeitika wito afande,"


Kamishna sasa akanyanyua kichwa chake ambacho kilikuwa bize kuendelea kusoma yale maelezo katika lile kalabrasha lililoandikwa na Fatma!,


"Nimekuita kwa maana,nataka nikukabidhi zingatio lingine japo la awali ujalikamilisha,utajua jinsi ya kufatilia na vijana wako,pitia hili faili ripoti zote za uchunguzi utaniletea mimi,kwa sasa una mafaili mawili katika mkono wako kazi ipo juu yako"


Kamishna aliongea huku akimkabidhi Jona kalabrasha lile,Jona akalipokea na kuanza kulisoma!


Baada ya kulisoma na kulielewa si ndo akachukua picha aitazame sura ya huyo mtu alopotea.


Ile anaitazama akuamini alichokiona!,


Macho ya mshangao yakamtoka,sura ile aikuwa ngeni machoni mwake,aliikumbuka fika,akajikuta mikono ikimlegea na kushindwa kuishika vizuri ile picha,


Akaiachia!..


Mshangao aloupata ulimshangaza Nurdin na hata Fatma,kwa uzoefu wao wa kipolisi walijua tu kushtuka kwa inspekta yule kuna sababu!


"Vipi inspekta mbona umeshtuka au unamjua mtu huyo?!"


"ha..ha..hapana mkuu!"


Jona akajikuta akipatwa na kigugumizi kikali,kamishna akawaruhusu, wakanyanyuka na kila mmoja akatoa heshima kwa mkuu wao,wakageuka na kuufata mlango kalabrasha lile sasa likiwa mkononi kwa Jonathan,walifika mapokezi,Jona akampa pole yule mama.


"Usijali mama hakuna lolote litakalo wapata na nikuhakikishie tutawakamata wauaji kuwa na amani mama yangu"


Jona aliongea kwa majonzi,kama vile ajui kitu,palepale akamwomba Fatma pamoja na binti mwingine kruta waelekee nyumbani kwa yule mama wakawe walinzi kwa muda,walichukua namba za ile gari,baada ya kuondoka ndipo Jona alipowapa ile picha wenzake ambao nao walishtuka vilevile,wote wakasoma kalabrasha lile na kulielewa vizuri!..


Kumbe huyu jamaa alikuwa ni mfanyakazi wa ofisi ya Raisi!,ila hawakuwa na shaka kuwa pia alikuwa ni muuzaji wa madawa ya kulevya!


Ilikuwa lazima wamjulishe inspekta Butu juu ya jambo lile haraka iwezekanavyo,hawakutaka kusubiri tena usiku kukutana Kivulini Bar.


Inspekta Jona akashika simu yake na kutafuta namba za Butu akazipiga,simu ikaita punde ikapokelewa.....


***


Butu furaha ilienda mbali na yeye,majonzi yalimtawala,alizidi kugida bia kwa uchungu,katu akujua kila anachofanya mwanaume wa kazi Zidu kite alikuwa akifatilia katika simu yake alounganisha na camera ndani ya nyumba ile!


Nje ya nyumba yake,mita kadhaa usawa wa barabara,ni muda mrefu alionekana binti mmoja kichaa pembeni ya mtaro akiwa na pochi lake chafu


Macho ya kichaa yule yalikuwa eneo la geti ilipo nyumba ya Butu!


Pia mtaa wa pili kutoka mtaa ule katika moja ya restraunt ilipaki pikipiki

ambayo ilikuwa ikimilikiwa na kijana mmoja alokuwa ndani ya gwanda za jeshi macho yake yalikuwa bize na tv ilokwepo pale.


Ni toka asbuh mjeda yule alikwepo pale.


Na siyo siku hiyo tu,


Hapana!!!....


Alishamaliza wiki alikuwa akija asubuh na kukaa pale mchana alikula pale usiku alikula pale saa tatu ndipo alipo ondoka


Butu pale sebuleni aliendelea kugida bia ghafla akapata wazo,muda ule ule mwanaume akajinyanyua na kufungua mlango,akatoka mpaka nje na kuchukua pikipiki yake,akaiwasha alipofikia getini akashuka akafungua geti na kutoka,ile katoka tu,yule kichaa akaingia ndani ya mtaro akawasiliana na yule mwanajeshi ambaye mara kibao kwa siri sana alikuwa akimfatilia Butu.


Baada ya mjeda yule kutaharifiwa alitoa simu yake na kumpigia Zidu.


"Mtu wetu katoka bad garl kanambia sijui anaelekea wapi ila ndo namfatilia"


"Nami nakuja akikaa position nzur mwangamize tu amri ishatoka"


Zidu kule nyumbani alinyanyuka naye akapakia tukutuku lake akatoka,silaha kibindoni!,alizidi kuwasiliana na yule mjeda kupitia vinasa sauti kutoka kwenye simu 'earfone' zilizopo masikioni mwake!


Butu alizidi kukanyaga mafuta pasina kuwa na shaka na mwanajeshi alokuwa akimfata nyuma akiwa juu ya pikipiki,


Mwanajeshi yule hakuwa mwingine zaidi ya Isack


"Ukifika usawa wake hakikisha kwa siri sana unammiminia risasi na kutoweka fastar hakikisha uachi ushahidi utakaowezesha kukamatwa kwako!"


Zidu akampa taharifa Isack ambapo alizidisha kasi ya pikipiki yake mpaka akamfikia butu akamuovar take sasa wakawa katika usawa,Isack sasa akaachia mkono mmoja na kuupeleka kibindoni akaanza kuhesabu moja.. mbili..tat..


Akiwa na nia akikamilishe 'u' achomoe pistol na kumaliza kazi palepale!....


*HATARI*


KIZAAZAA....

ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

BLOG