Search This Blog

Saturday, February 26, 2022

GENGE - 3

    *

Simulizi : Genge 

Sehemu Ya Tatu (3)



Nje tu ya mlango wa kile chumba, Dastani alikuwa keshaikamata sawia bastola yake. Moyo ulimwenda mbiyo, akapumua kwa nguvu. Aliupata vyema ujumbe wa Aziza kuwa afike wakati huo.

“Nimefika Darling, niko mlangoni…” akajibu kana kwamba Aziza anamsikia kumbe la. Pigo moja la nguvu, lakaufungua mlango. Dastan akaruka sarakasi upande wa pili. Aziza akamkumbatia kwa nguvu Bambros na kujigeuza naye ili amweke sawa upande wa Dastan. Haikuwa rahisi. Bambros aliijua vyema michezo hiyo, alimgeuza Aziza kwa mtindo wa ajabu akidhamiria kama ni risasi basi imuue mwanamke huyo. Wakati huo huo, mkono wake mmoja ulipita kama umeme chini yam to na kuinyakua bastola yake. Alimbwaga Aziza chini, lakini kabla hajaifyatua risasi yake kumwelekea Dastani, akajikuta akipaishwa juu na kubwagwa upande wa pili kama mzigo, macho yamemtoka. Dastan hakua na muda wa kupoteza, akainuka na kuytakua ile briefcase, akatumbukiza kila karatasi lililokuwa juu ya meza ndogo bila kusahau kabatini.

“Vaa nguo Aziza tuondoke chap-chap!” akamhimiza.

Sekunde chache zilizofuata, wakawa tayari ngazini wakiteremka chini. Wakaingia garini na kuondoka kwa kasi.

“Mwanaume una shabaha!” Aziza akamwambia Dastan wakati akifunga vifungo vya blauzi yake.

“Ndiyo kazi yangu,” akamjibu huku akibadili gia na kuweka namba tano.

* * *

“Ndivyo alivyotufanya,” Big J akawaambia wenzake. Ukimya ukajidai kati yao kila mmoja akiwa hana la kusema.

“Msiumize kichwa, nani anatufuatilia,tutamjua tu. Na tukimjua hakuna mswalie Mtume… ni risasi ya kichwa!” Mc Tee akawaambia.

“Sitaki kuamini kuwa wanatuzidi nguvu au maarifa. Big J, we unawajua sana wale, hebu tufanyie utafiti tujue nani anayetutikisa ili tumfanyie kazi. Au la wamekodi mtu,” Bi. Jesca akamwambia Big J.

“Huu si muda wa kujitokeza mama, tumeshabaki wawili, cha kufanya… kama Mc Tee alivyosema, tungoje. Ila azma yetu mwaka unaokuja lazima itimie. Tutaichukua nchi, iwe kwa damu au kwa maji,” Big J akajigamba.

Kikao hakikuwa kirefu lakini kilijawa na maamuzi mazito. Mc Tee, Big J pamoja na Bi. Jesca waliamua kuongeza nguvu, kukodi vijana maridadi watakaoweza kupambana na wana usalama wa serikali pindi tu wakiamua kuwafuatilia.

* * *


Dar es salaam – Shamba


Kamanda Amata na Chiba walikuwa ndani ya chumba maalumu cha utambuzi. Karatasi kadhaa zilizoandikwa mambo mengi kwa kalamu nyeusi zilitapakaa mezani. Wakati Chiba akiwa ametingwa, macho kodo kwenye kioo cha kompyuta; Amata alikuwa akipekuwa karatasi hii na ile, akiandika hapa na pale.

“Vipi umegundua kitu?” Amata akamuuliza Chiba bila kumtazama.

“Mambo mengi mazuri. Hawa jamaa wana mpango mbaya sana kwa nchi hii. Na mpango huu kaka, umesukwa kitaalam kweli kweli. Mpaka sasa tumewaangushan Mwakibinga na Mwanachia lakini kuna gepu kubwa kati yao na Mtokambali na Msambamagoya,” Chiba akamwambia Amata.

“Kivipi?” Amata akamuuliza Chiba huku akiacha kile alichokuwa akifanya.

“Maelezo na vielelezo vyote kutoka kwenye hii hard disc uliyopileta vinaishia kwa hao wawili tu. Hakuna kinachomgusa Mtokambali wala Msambamagoya. Zaidi kuna mambo mengi ambayo nashindwa kuyaelewa yanataka kunieleza nini. Inaonekana ndani ya taarifa hizi kuna taarifa za siri ndani yake…”

“Unataka kunambia kuna kitu kimefichwa?” Amata akamkatisha maelezo kwa kumchapa swali.

“Ndiyo!” akamjibu.

Amata akainuka kutoka pale alipoketi, akachukua kiti kingine pamoja na kitabu chake cha kuandikia kumbukumbu, “Enhe!” Akamtaka kuendelea. Wakati Chiba anaendelea kuelezea kile anachokiona kwenye kompyuta yake, Amata alikuwa bize kunakili hiki na kile.

“Sikia Chiba, hawa jamaa wanauelezea mpango wao kwa mafumbo sana. Inabidi tutulie kujua nini kimefichwa,” akamwambia na Chiba akatikisa kichwa kuafiki.

“Kwa haraka haraka, hii taarifa ipo nusu, inabidi tuipate nusu nyingine ili tuikamilisha,” Amata akamwambia Chiba na kutua kalamu yake mezani.

“Kibarua asee, yanarudi yaleeee ya Dassen Keputo,” Chiba akasema na wote wakacheka.

“Taarifa ya mwisho ambayo alikuwa akiiandika Bwana Vincent Mwanachia, inahusu mapokezi ya mzigo…” Chiba akaeleza.

“Mzigo gani?”

“Haijaelezwa ni mzigo gani ila tu imesema ‘mzigo utapokelewa palepale tulipokubaliana muda wa shetani’ basi,” akaeleza.

“Na ukirudi nyuma kuna taarifa gani zaidi?” Amata akataka kujua.

“Hukutakiwa kumwacha Dana aisee, inaonekanaana mengi anayoyajua kwani hapa naona picha ya pamoja,” Chiba akamwambia Amata. Akainakili ile picha, akaiingiza kwenye softiwea yake ya utambuzi na kuanza kufanya kile ambacho kitaalamu kinaitwa foresinc investigation.

Katika picha ile, kulikuwa na watu watano. Ile softiwea ikamtambua haraka Dana, kisha

Mwanachia. Haikuweza kuwatambua watatu waliobakia, ambao kati yao kulikuwa na mzee wa Kizungu aliyevalia suti ya gharama sana na vijana wawili pia Wazungu. Upigwaji wa picha ile ulionesha wazi kuwa ilipigwa baada ya kikao fulani.

“Fanya uwezalo tupate jina la huyo mzungu na mahali walipopiga hiyo picha,” Amata akasema wakatia akiichukua nakala ile kwenye mashine ya kuprinti.

“Nipe dakika kumi tu,”

“Ok!”

Chiba, TSA 2, mshititi katika kile kinachoitwa Cyber intelligence na Foresinc Investiation, aliijua vyema kazi yake. Alikuwa na kila zana ambayo ingemrahisishia uchunuzi wake, iwe kwa kompyuta au kifa kingine chochote kile. Akaiweka kwenye kioo kikubwa picha ile. Kwa kutumia kipanya cha kompyuta hiyo kubwa. Akakata sura ya huyo aliyemtaka kisha akaihamishia katika kiboksi kingine na kukiamuru kifanye kazi yake. Upande wa kushoto wa kidirisha hicho kukatokea majina yanayopita kwa kasi sana. Upande wa kulia, kulionekana usanisishaji wa viungo vya kichwani kama pua, masikio, midomo, macho ili kuona ni kipi kitaweza kuoana na picha ile. Dakika mbili zilipaita na baadaye kila kitu kikasimama lakini bado upande wa kulia haukuleta majibu sawasawa, mambo hayakuwa mukashara.

Macho hayakuoana, lakini kope zake zilienda sawa kabisa na picha hiyo. Masikio hayakuoana sawasawa hasa la upande wa kushoto. Jina lililosimama upande wa kushoto, lililomeka Mr. Sebastiano Moznich, raia wa Italia, Jiji la Toscana. Maelezo yalienda mbali zaidi, ni mfanyabiashara wa magari ya Ferrari.mwenye makazi yake katika jiji hilo hilo.

Kamanda Amata aliitzama ile picha kwa makini sana, wakati huo Chiba alikuwa ametingwa kwenye kompyuta yake.

“Sebastiano Moznich! Ni nani katika mchezo huu?” Amata akauliza.

“Huyu ndiye key point kwa sasa, lazima aje shamba,” Chiba akasema.

“Sawa, kingine…”

“Siri ya wapi Msambamagoya na Mtokambali wamejificha,” Chiba akamjibu. Kamanda Amata akachomoa bahasha moja ndogo na mara baada ya kuifungua ndani yake, akatoa nakala mbili za picha za black and white. Moja ilimwonesha Msambamagoya James na nyingine Mtokambali Kibwana. Picha hizi zote ziliandikwa kwa nyuma; moja 1980 na nyingine 1979.

“Mpaka sasa watakuwa wameshabadilika sana,” Chiba akamwambia Amata wakati akizitazama zile picha.

“Ndiyo, kwa sasa inabidi tuzitengenezee uzee ili tupate taswira ya mwonekano wao kwa sasa,” Amata akasema.

“Nimekupata,” akajibiwa. Muda huo huo Madam S akaingia ndani ya chumba hicho maalum. Akawakuta vijana wake wakiendelea na kazi.

“Huyo ni nani?” akauliza akiwa anaitazama ile picha pale kwenye liuninga.

“Sebastiano Moznich!” Amata akajibu. Madam S akasogelea zaidi kile kioo, akaitazama ile picha, kisha akamgeukia Amata, “Anahusika?”

“Hatuna uhakika ila turufu yetu imeangukia kwake… hatumhukumu ila tunamtuhumu. Uchunguzi unaendelea,” akaeleza, “Ila Dana anahitajika hapa kwa mahojiano”.

“Haina shida, nitawasiliana na bosi wake, atapatikana tu,” Madam akajibu. Alipomaliza kauli yake, akaangalia na zile nyingine kisha akasoma na maelezo kadhaa yaliyo ndani ya luninga ile.

“Naona mmekwama vijana… ushauri wangu ni mmoja tu na ni ambao nimeufikiria sasa hivi…”

“Enhe…” Amata akamkatiza kwa kushadadia.

“Tusiumize kichwa na hawa watu wawili wakati familia zao zipo hapa mjini. Upelelezi wetu uanzie hapo na baadaye tutapata fununu za kujua ni wapi wamejificha,” akawaambia.

Chiba na Amata wakaafiki na kubaki wakitazana. Hawakuwaza!

Yaani tunawaza vitu vikubwa wakati vidogo tunavisahau! Amata akawaza.

“So?” akamuuliza Chiba.

“Bado nahitaji kumchunguza zaidi huyu jamaa…”

“…nani?”

“Sebastiano. Lakini kama tulivyokubaliana, inabidi tuzigeuze hizi picha kuwa za wakati huu,” Chiba akakumbusha.

* * *

Siku hiyo hiyo, wakati TSA wanaendelea na uchunguzi wao huko Shamba, Mc Tee, Big J na Bi Jesca walikuwa wakihitimisha zoezi lao la utambuzi.

“Vipi?” Bi Jesca aliuliza alipowaona wanaume hao wakirejea vitini. Giza lilikwishaanza kuimeza nchi na muda wa kikao chao ulipitiliza kiasi kwamba kila mmoja wao akawa na wasiwasi na usalama wake.

Mc Tee akaiweka kompyuta yake ndogo mezani, “tumepata jibu” akasema.

“Enhe!” Jesca akadakiza kutaka kujua.

“Hizi alama za vidole katika hii kompyuta ni za mtu hatari sana. Serikali ya Tanzani imeanza kukodi wapelelezi hatari dhidi yetu,” Mc Tee akawaambia wenzi wake.

“Inawezekana. Maana kama angekuwa mwanausalama wa kawaida ningemjua tu, au watu wangu wangemjua lakini wamekiri kuwa TNS hawana code 005” Big J akaeleza.

“Code 005! Inamaanisha nini?” Jesca akauliza.

“Katika utambulisho wa namba za kiusalama kwenye mashirika ya kijasusi, hii code humaanisha mtu hatari kuliko hatari yenyewe. Mwenye uwezo mkubwa wa kufikiri na Sanaa ya mapigano ya kiwango cha juu,” Big J akaeleza.

“Mh!” Jesca akaguna, “Nitakwenda Dar es salaam kwa siri nitawapa jibu kuwa ni nani…” akasema.

“Hilo si wazo jema hata kidogo, kumbuka wewe umeshatikisa nchi kwa maneno yako makali.

Wanakufahamu kwa matusi yako, maandamano uliyoyaitisha yakaitikisa serikali hayajasahaulika.

Wanakusaka, usalama wako tuni kwamba serikali ya Marekani inakulinda kwa namna fulani. Usijaribu kuikanyaga ardhi ya Dar es salaam, wakikugundua hawatakuacha na pumzi yako… be carefull mammy,” Big J akamweleza Jesca. Mwanamke, mwanaharakati aliyeweza kuitikisa serikalikwa maneno yake. Mwenye siri nzito nzito za vigogo, kuanzia za chumbani, sebuleni mpaka ofisini. Alitisha.

“Najua nitakachofanya, mimi ni mwanamke, siogopi kitu…” akawaambia akijipigapiga kifua.

“Angalia sana! Serikali ya Tanzaniainakusubiri kwa hamu sana utie mguu wako wakunyakue. Naogopa na usifanye hivyo. Tunaandaa kikao maalumu, safari hii ni kuwaalika viongozi wa vyama mbalimbali vya siasa ili tuwasikilize mikakati yao kisha tutumie mwanya huo kupenyeza ajenda zetu…” Mc Tee akawaambia Big J na Jesca.

“Lakini, pamoja na hilo, tunafisha juhudi zetu…?” Big J akauliza huku akijikuna kichwa chake.

“No! Hatufishi. Katika mazungumzo na God Father, amahakikisha kutusaidia kila kitu ilimradi tutimize lengo letu. Ndipo nikakaja na wazo jipya ambalo tungeweza kuliunganisha na lile la msingi. Halafu kwa yote pamoja tutapata matokeo mazuri sana, mtafurahi,” akawaeleza.

“Sawa , tutaweka mipango vizuri ili kila kitu kiwe sawa. By the way, taarifa zaidi za huyu bwana 005 tutazijua tu muda si mrefu. Nimeshazituma kwa mtu wetu,” Mc Tee akaeleza.

“Hatuna shaka na hilo, tukishamjua tu, kazi imeisha. Tutamuua kimya kimya na kuuyeyusha mwili wake kwenye tindikali,” Big J akaongeza kusema.

Kikao cha watu hawa watatu kilihitimishwa. Jambo moja tu lililokuwa likisubiriwa ni ufafanuzi zaidi wa code iliyojitokeza, ambayo wao walikosa kuielewa kwa undani kuwa ni nani inamwakilisha kwa jina, cheo na wajihi wake.


KICHWA CHA MADAM S hakikupata wasaa wa kutulia. Jambo gumu na kubwa liliendelea kumsumbua kichwani.

Tunakwama wapi? Akajiuliza. Usiku huo alilala chali kitandani, akiwa na vazi la kulalia tu. Taa yenye mwanga wa rangi ya orange iliyowekwa kwenye meza ndogo ilikijaza chumba hicho kwa uhafifu wake. Ungeweza kumletea usingizi, lakini kwake haikuwa hivyo, tuli, alitulia. Alihakikisha ananyamazisha kelele zote ubongoni mwake ili achambue kimoja baada ya kingine.




KICHWA CHA MADAM S hakikupata wasaa wa kutulia. Jambo gumu na kubwa liliendelea kumsumbua kichwani.

Tunakwama wapi? Akajiuliza. Usiku huo alilala chali kitandani, akiwa na vazi la kulalia tu. Taa yenye mwanga wa rangi ya orange iliyowekwa kwenye meza ndogo ilikijaza chumba hicho kwa uhafifu wake. Ungeweza kumletea usingizi, lakini kwake haikuwa hivyo, tuli, alitulia. Alihakikisha ananyamazisha kelele zote ubongoni mwake ili achambue kimoja baada ya kingine.

Mwanamama huyu alikuwa mbobevu sana katika maswala ya kijasusi, daima alijua anachofanya. Uongozi wake katika kitengo cha siri cha serikali ulitambulika vyema na Mkuu wan chi, aliheshimika kwa siri vilevile. Kazi yake ilionesha matunda. Vijana wake hawakumwangusha. Mpaka siku hii alipojilaza kitandani, uzee ulikuwa unapiga hodi. Mvi zilikijaza kichwa chake na kumfanya awe mrembo maradufu. Hakuwahi kuolewa. Ijapokuwa alikuwa na mabwana wa hapa na pale ili kukata kiu yake ya kike, bado hakuwahi kupata mtoto. Si kwamba alikuwa tasa, la, ila majukumua na kazi yake vilimfanya aepuke kushika mimba. Haya yote yalimpa mawazo mengi kadiri umri ulivyokuwa ukienda. Watoto pekee aliyewaona ni wake ni vijana wa TSA na si wengine. Aliwaita wanangu, nao wakamwita mama.

Akili ya Madam S ilizimika na kuacha giza nene katika ubongo wake. Hii alijifunza huko Mongolia katika pitapita zake za mafunzo ya Kiintelijensia. Akarudisha kumbukumbu moja moja za nyuma. Kumbukumbu zake zikamrudisha alipokuwa na umri wa wastani. Siku alipopokea barua ya kutakiwa kuripoti Ikulu katika kitengo cha usalama.

Alipokelewa na watu wawili wacheshi ambao aneweza kumwita mmoja baba na mwingine baba mdogo. James Msambamagoya na Chameleone, walimpokea, wakampa ofisi na kumsimamia kwa ukaribu sana katika kazi waliyompa. Selina akafanya vizuri, aliweza kuratibu vyema safari za ndani za Rais, kupanga makabrasha na mambo mengine ya kiitifaki. Alimheshimu sana Chameleone kwa jinsi alivyokuwa akipanga mambo yake. Akajitahidi kujifunza na kuiba mambo kadhaa. Akafanikiwa. ‘Binti Chameleone’ wakampa jina. Kwa sababu mwishowe alikuwa na tabia kama za mzee huyo. Hakuwa na ukaribu sana na James Msambamagoya, kwa kuwa alimtaka kimapenzi mara kadhaa.

“Sikiliza binti… nakupa kazi ya siri, na uifanye kwa umakini”. Sauti ya Chameleone ilimrudia kwenye kumbukumbu zake.

“Nahitaji umfuatilie au umchunguze James… ila uwe makini sana asijue hili. Nataka unambie, akimaliza kazi hupendelea kwenda wapi, na nani ikiwezekana nipe hata orodha ya marafiki zake anaokutana nao mara kwa mara.” Agizo.

Madam S aliikumbuka siku hii, jinsi alivyoweza kumfuatilia mwanausalama huyo. Aligundua kuwa, baa aipendayo ni Banana. Aliwatambua marafiki zake, aliokuwa anakunywa nao. Wanajeshi. Sura zao aliziona mara kadhaa walipokuwa wakija Ikulu kwa kazi maalumu. Alivuta sura ya mmoja mmoja, alikumbuka wapo waliofungwa kwa kesi ya uhaini, wengine walitoroka. Kati ya waliotoroka alikumbuka Mwanachia aliyejulikana kwa jina la Chatu, alikwishauawa. Alimkumbuka Mwakibinga naye alikwishauawa kwa mkono wa TSA. Bado wawili.

Yuko wapi aliyekuwa waziri wa mambo ya nje wakati ule? Ambaye iligundulika kuwa ndiye mpanga mipango, anayeitaka nchi, aitwe rais. Uchu wa madaraka.

Madam S alikuwa bado kitandani, chali. Akili yake ilikuwa imepaa mbingu ya saba, nje ya upeo wake wa kawaida. Iliitaji utulivu mkubwa kuweza kuwasha sakiti mpya ya umeme katika ubongo, kucukua tafutishi kutoka kwenye memori za muda za wakati huo. Kutafuta wapi zilitupa kumbukumbu hizo na kuzirudisha kwenye mfumo wa LTM yaani Long Time Memory. Ni zoezi gumu ambalo majasusi ujifunza. Katika zoezi hili mfumo wa kumbukumbu wa Madam S ulirudi kwa Chameleone.

“Nina ofisi yangu ya siri ambayo taarifa nyingi zinapatikana…” sauti ya Chameleone ilimrudia kichwani.

Hospitali ya Ocean Road! Akajikuta akiwaza.

Ding! Dong! Sauti ya kengele ilimgutua. Akafumbua macho na kushusha pumzi kwa nguvu.

Ding! Dong! Ikajirudia tena. Haraka haraka, akachukua kitabu chake cha kumbukumbu. Akafyatua kalamu na kuandika mambo machache muhimu. Akakiacha kitanda na kuliendea kabati la nguo. Akachojoa na kuchukua koti refu na kujitupia mwilini. Akafunga zipu yake mpaka chini. Akaenda sebuleni na kuwasha taa. Alielewa ni nani anayegonga mlangoni kutokana na jinsi alivyoibonya kengele hiyo.

Kabla hajafungua geti akatazama saa yake. Saa sita kasoro robo usiku. Akafungua geti.

Kamanda Amata akajitoma ndani na Madam S akafunga geti lile. Hatua chache wakafika sebuleni, pombe kali ikawekwa kati. Wote wawili, kila mmoja, akajitupa kitini.

“Yes Kamanda!” Madam S akamsabahi kwa namna hiyo mara baada ya kushusha bilauri yenye kinywaji.

“Madam, akili yangu haijatulia kabisa…” akasema na kupiga tena funda moja la kinywaji kile.

“Nini unafikiri?” Madam akamrudishia swali.

“Madam nimetoka kuachana na mtoto wa Mtokambali, nililoambiwa sijalitegemea,”

“Nambie mwanangu…”

“Kibwana Mtokambali alikwishafariki na amezikwa huko Kiev,”

“Nani amekwambia?”

“Mtoto wake wa kwanza, Bwana Onesmo anaishi Mwananyamala,”

“Umeonana naye?”

“Ndiyo, nilimtafuta nikampata nyumbani kwake, nikazungumza naye mengi sana. Anailaumu serikali kwa kutomjali baba yake. Anauliza, ukiachana na kosa alilohukumiwa kama mhaini mbona mmeusahau utumishi wake kwa miaka yote?” Amata akaeleza. Kutoka mfukoni mwake akachomoa rekoda ndogo, akawasha. Wote wawili wakaanza kusikiliza mazungumzo yale kutoka Alfa hadi Omega.

* * *


KIEV 1980


Katika Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Boryspil Kyiv, Kibwana Mtokambali alipokelewa na swahiba wake Colonel Ivan Chernyakhovsky. Colonel huyu alimfahamu vyema Kibwana Mtokambali kwa kuwa walikutana kwenye mafunzo ya kijeshi mwaka 1968 huko katika Akademia ya Kijeshi ya Kiev. Ivan alijua fika nini dhamira ya swahiba wake. Tangu wakiwa katika academia hiyo, Mtokambali hakuweza kuficha hisia yake.

“Utakuwa mwanaume kamili ukifanikiwa hilo, hata ukishindwa, utakuwa umejaribu pakubwa…” Ivan alimwambia mara kadhaa wakiwa katika mafunzo yao. Tofauti na Kibwana, Ivan yeye akili yake yote ilikuwa ni kuanzisha chuo cha maswala ya usalama katika Kiev. Ndoto yake haikufa mpaka alipofanikiwa kwa asilimia kubwa na serikali kumsaidia.

Siku hii, ndani ya uwanja wa ndege alimpokea shujaa wake huyu.

“Tovarishch, ya ne smog…” Kibwana akamwambia Ivan kwa Kirusia kuwa ameshindwa jaribio lake.

“Ne volnuysya, moy pokazhu tebe drugoy put,” brat. YA Ivan akamtoa wasiwasi na kumwahidi kumwonesha njia nyingine ya kufanikisha lengo hilo. Wakakumbatiana kwa sekunde kadhaa kisha wakaelekea garini ambako mizigo yote ilikuwa tayari imekwisha pakiwa.

“Karibu tena Kiev komredi…”Ivan akamwambia Mtokambali.

“Nimekaribia, asante sana…”

Wote wawili wakaondoka uwanjani hapo kwa gari maalum la kijeshi. Baada ya mwendo wa takribani dakika arobaini na tano, waliwasili katika kitongoji kimoja mashambani. Lile Fiat likaingizwa ndani ya wigo mkubwa uliuzungukwa na kila aina ya ulinzi. Jumba la kifahari lilikuwa katikati ya wigo huo. Mara tu alipokanyaga ardhi, Kibwana akapokelewa na mwaDanada mrefu wa wastani, mwenye nywele nyeupe zilizomwagika mgongoni mwake. Suruali yake ya kijeshi ilimkaa vyema na kumpendezesha haswa.

“Kutana na Barbier Saratov,” Ivan akamwambia mgeni wake.

? “Nafurahi kukutana nawe Barbier…”wakasalimiana na kuzungumza machache kisha wakaelekea ndani ya jumba hilo. Moja kwa moja walifikia katika meza kubwa ya chakula, iliyopambwa na pombe kali kali. Kijindoo kidogo chenye barafu kilikuwa kikifuka mvuke. Kibwana Mtokambali aliitazama ile meza na kukumbuka miaka ya nyuma alipokuwa katika nchi hiyo kwa mafunzo ya kijeshi. Katika meza hiyo kulikuwa na watu watatu tu, Ivan, Barbier na Mtokamba. Akukuwa na mtu mwingine na wala hakukuonesha dalili ya kuwa na mtu wa ziada katika jumba hilo, ukiachana na walinzi wa nje.

Baada ya glasi mbili tatu kumiminiwa tumboni, ukimya ulivunjwa.

“Kwa katiba ya nchi yetu, nitahukumiwa kifo,” Kibwana alimweleza Ivan.

“Kamanda haogopi kufa, kwa kuwa ni sehemu ya maisha yake hasa anapopigania taifa lake,” Ivan akajibu.

“Najua comrade!”

“Sasa wasiwasi wako ni nini?” Ivan akamuuliza swahiba wake.

“Sina wasiwasi,”

“Hayo ndiyo maneno. By the way, utakuwa na Barbier kwa takriban wiki tatu au mwezi hivi. Yeye atakupitisha katika michakato tofauti ya kukubadili na kukurudisha tena kwenye uwanja wa vita,” Ivana akamwambia Mtokambali.

“Kunibadili?” akauliza.

“Naam, wewe utahukumiwa kufa, na utakufa, sasa sisi tunakuua mapema na kukurejesha vitani,” akamweleza, “Barbier!” akaita.

“Yes Sir!”

“Mweleze kinachoendelea kwa ajili yake,” Ivan akamwambia yule mwanamke. Barbier akavuta droo kubwa chini ya meza hiyo, akatoa kabrasha moja na kuliweka mezani. Alipoifunga ile droo, akalifungua lile kabrasha. Ndani yake kulikuwa na karatasi kama kumi hivi zote zikiwa na sura za watu, wazungu na majina yao. Zaidi ya hapo kuliokuwa na tarakimu nyingi sana.

“Nani unampenda kati ya hawa?” Barbier akamuuliza Mtokambali huku akimsogezea lile kabrasha. Mgeni huyo akachukua lile kabrasha na kuanza kulipekuapekua. Picha namba kumi na moja, akaipenda. Akamrudishia Barbier lila kabrasha kama alivyopewa, yaani kwa kulisukuma.

“Ok!” Barbier akatamka. Akaitatua ile karatasi na kuondoka pale mezani akiwaacha Mtokambali na Ivan, marafiki wawili.

“Don’t worry Kibwana. Hakuna linaloshindikana chini ya jua, utaona tu. Mimi na watu wangu tutakupa kila kitu ili ufanikishe lengo. Mafanikio yako ndiyo yetu kama tulivyopanga,” Ivan akamtoa wasiwasi.

Dakika kumi baadae, Barbier alirudi na kuketi katika kiti kilekile.

“Kila kitu sawa?” Ivan akamuuliza.

“Ndiyo! Kinachofuata ni kujiandaa kwa safari wiki moja ijayo. Dakta Punchkunel yuko tayari na atakuwa kwa ajili yetu siku hiyo,” Babier akatoa maelezo. Wakati yuote haya yakionelewa, Kibwana alikuwa kimya akigugumia vodka yake. Hakuna alichokielewa zaidi ya kusikia tu.




Dakta Punchkunel yuko tayari na atakuwa kwa ajili yetu siku hiyo,” Babier akatoa maelezo. Wakati yuote haya yakionelewa, Kibwana alikuwa kimya akigugumia vodka yake. Hakuna alichokielewa zaidi ya kusikia tu.


* * *


Dar es salaam


Madam S aliegesha gari nje ya hospitali ya Ocean Road. Asubuhi ya siku hii, mvua ya rasha rasha ilikuwa ikiendelea kunyesha. Akiwa ndani ya koti kubwa la mvua, akavuta hatua kuelekea jengo moja dogo lililotelekezwa kando tu mwa ukuta wa hospitali hiyo. Mmea mkubwa wa mpaseni ulikuwa umefunika jengo lote. Unetazama tu unejua wazi kuwa hakuna aliyekuwa akilitumia kwa kipindi kirefu. Alipolizunguka upande wa pili akakutana na mlango mdogo uliosonwa na mpasheni ule. Akasimama kwa jozi la sekunde akitazama vizuri ule mlango. Akajipapasa mfukoni na kuchomoa funguo moja aliyoona inamfaa kwa kazi hiyo. Akasukuma huku na huko mpasheni ule na kufanikiwa kupachika ufunguo. Alipouzungusha, kitasa kile cha kizamani hakikuleta ubishi. Akausukuma ndani kwa nguvu kidogo. Mlango ule, ukakwangua chini kutokana na uchakavu wake. Alipopata upenyo wa kuingi akafanya hivyo. Akaurudisha kwa tabu vilevile na kujikuta kasimama kwenye chumba kidogo.

Ndani ya chumba hiki kulikuwa na meza moja nzuri ya mninga. Ilimstaajabisha Madam S kwa usafi wake. Tofauti na alivyotegemea kuwa angekuta buibui na wadudu wengine, haikuwa hivyo. Ofisi ile ilikuwa safi, picha ya Chameleone ilikuwa ukutani ikining’inia. Madam S alishangaa, akatazama huku na huku akitegemea labda atasikia sauti ikimwita.

Nani husafisha humu ndani? Akajiuliza.


Alipoona hilo halina majibu akapitisha macho yake kwenye rafu ya vitabu na makabrasha iliyosimama mbele yake. Akatia mkono kupekuapekua kama aneweza kuona chochote ambacho kingemsaidia. Madam S alijikuta anapekua kila kabrasha. Ndani yake alikutana na mambo mengi sana, mabaya na ya kutisha. Siri nzito nzito za na mipango ya hatari isiyofaa kuonwa kwa macho mepesi. Madam S alijikuta akitetemeka mikono kama mtu anayepiwa na baridi.

Nani anatumia ofisi hii? Akajiuliza mara nyingine. Unafuu ulipomrudia akasogelea tena rafu ile. Mwili ukasisimka, nywele na vinyweleo vikamsimama pindi tu alipokama kabrasha moja lililoandikwa Most Wanteds. Akiwa katika kulivuta, ikaanguka picha moja ya wastani. Macho ya Madam S yakaiona sura ya James Msambamagoya. Akapata shauku ya kufunua zaidi. Kulikuwa na kurasa kama hamsini hivi zenye picha na maandishi. Hakupenda kupoteza muda katika ofisi ile. Akalifutika kabrasha lile kotini na kutoka nje. Mara hii mvua ilikuwa kubwa zaidi. Alipoufunga tu mlango akakimbia kulielekea gari lake. Akafungua mlango na kuketi ndani yake. Akashusha pumzi ndefu na kulivua lile koti, kisha akalitupia kiti cha nyuma. Lile kabrasha akalipachika kati ya kiti na kiti ambapo si rahisi mtu kujua. Akatia moto injini na kuondoka taratibu kutoka katika yale maegesho. Mapigo ya moyo yalikuwa yakimwenda kasi, hali iliyokuwa ikimtia wasiwasi.

Kuna kitu! Akawaza wakati akiingiza gari katika maegesho ya Chuo cha Magogoni. Akazima gari na kusubiri sekunde kadhaa akitazama vioo vyake vya pembeni na kile cha ndani ili kuona kama kuna anayemfuata. Alipojiridhisha kuwa usalama upo wa kutosha, akateremka na kabrasha lile mkononi. Kwa kutumia njia zake za siri, alipita mpaka Ofisi Ndogo. Akalitua mezani na kulitazama bila kulimaliza.

Nina uhakika, siri zote nitazipata humu. Chameleone hakuwa mtu wa mchezo! Akawaza na kuizunguka meza mpaka upande wa pili, akaketi na kuliweka sawa kabrasha lile.

Most Wanteds!

Lilisomeka juu kabisa. Kwa mikono ya kitetemeshi, alifungua jalada lake na kukutana na ukurasa wa juu kabisa ulioandikwa kwa mkono Top Secret. Hii tu ilitosha kujua nini anaenda kukutana nacho. Macho ya Madam S yakatua kwenye kurasa ya pili. Ilikuwa karatasi ile iliyoandikwa tafutishi za mtu asiyejulikana. Tafutishi ambayo Chameleone alipewa na Mkuu wa nchi tangu mwaka 1980, iliyobeba majina ya watu wanaosadikiwa kuwa wana mpango wa mapinduzi. Mpango wa kumuua Rais ili kujitwalia madaraka. Katika kurasa hii ndimo alipokutana na orodha ile chafu. Majina asiyoyategemea ambayo yalivuma wakati yeye akiwa bado mpya kwenye medani ya usalama. Akaiweka pembeni. Akatupa macho kwenye kurasa ya tatu. Hapa akakutana na muhtasari wa kikao cha siri kilichokutanisha watu wa juu kabisa wa jeshi. Kikao kilichofanyika Banana Bar, Ukonga. Akaisoma kwa tuo bila papara. Katika kurasa hii, mpangomzima ulikuwa mezani, nani apewe cheo gani na cheo gani apewe nani. Huku ukimtaja Kibwana Mtokambali kama Rais wa nchi. Ilikuwa ni Syndicate hatari iliyoundwa na watu makini wanaoujua vyema uwanja wa vita. Madam S akatikisa kichwa. Mengi kati ya haya hakuyajua kabla.


Akafungua kurasa ya nne akakutana na orodha ya watu waliohukumiwa kifo baada ya kesi ile. Waliotoroka, wakawekewa alama nyekundu na picha zao zikielezea wajihi wao. Wengine waliofungwa maisha. Na wapo waliouawa. Picha zao zilikuwapo vilevile. Orodha ya chini ilikuwa ya wale wote walioachiwa huru.

Kurasa zilizofuata zilikuwa ni taarifa mbalimbali ya ufuatiliaji wa sakata hilo. Chameleone aliorodhesha njia zote alimopita katika upelelezi wake. Nani na nani alimhoji. Kipi na kipi alikipata. Akuishia hapo, aliweka majina mengine ambayo anayatilia shaka. Madam S hakutegemea kuyaona hapo.

Kurasa tatu za mwisho, zilitanguliwa na karatasi iliyobeba maandishi ‘Orodha Chafu’. Katika kurasa hizi kulikuwa na majina ishirini na mbili. Mpaka tarehe hiyo ambayo kabrasha hilo lilikuwa mikononi mwa Madam S, majina tisa yalikuwa na X nyekundu. Kila moja likielezewa sababu ya kuwekwa X hiyo, vifo. Madam S akavuta kumbukumbu na kung’amua kuwa majina hayo yote yalikuwa ya marehemu.

Kulikuwa na mauaji ya siri! Akawaza. Majina mengine hayakuwa na orodha yoyote isipokuwa manne ya mwisho. Haya yalifunikwa viboksi vyekundu na kuandikwa pembeni ‘Most Wanteds’. Maelezo yaliyofuatia chini yake ni kutaka watu hao wasakwe popote duniani na wauawe pasi na huruma. Madam S akaunganisha matukio ya kazi aliyopewa na Ikulu na hicho anachokiona.

Akagundua kuwa anatekeleza kazi ya Chameleone.

Akiwa katika kufunga kabrasha lile, akakutana na bahasha. Bahasha ile iliyobanwa kwa stepla pini iligongwa mhuri wa serikali wenye neno ‘SIRI’ katikati. Akaichana na kutoa karatasi mbili zilizokuwa ndani yake.

Moyo ulimpiga kwa nguvu, pumzi ikapanda na kushuka. Hakuamini anachokutana nacho.

Hati safi ya mkono ilikuwa imeandika taarifa hiyo fupi.


Wamesema wakimgundua mamluki yeyote anayekwamisha


juhudi zao watamuua bila huruma.


Ni mimi si mwingine, wataniua, lakini lazima niufikishe mpango huu dhalimu mikononi mwa serikali.


Mpango huu ni kigae katika choo changu cha ndani.

Na mengine mengi niliyoyakosa yapo katika nyumba namba 73A Kinondoni Mtaa wa

Galu. Nyumba hii ni mali ya Burushi mmoja mwenye urafiki wa karibu sana na

Kibwana Mtokambali…

Dastan Kihwelo


Madam S alijikuta akipandwa na hasira, alimfahamu kijana aliyeandika ujumbe ule. Dastan Kihwelo, aliyeuawa mara tu baada ya sherehe yake ya harusi. Hasira ziliwaka kichwani mwa mwanamama huyu. Akafunga lile kabrasha na kuliweka katika saraka yake ya siri ambayo ni yeye tu anayeweza kuifungua.



* * *


Mtaa wa Galu, Kinondoni

Sauti ya nukushi ilisikika kutoka katika nyumba namba 73A katika Mtaa wa Galu. Mbele ya mashine hiyo alisimama kijana mmoja mtanashati wa mavazi, mweupe wa rangi, na mrefu wa kimo. Mkono wake ulikuwa tayari kuinyakuwa karatasi iliyokuwa ikupokea ujumbe wa nukushi hiyo. Mkono mwingine ulikamata kikombe kidogo kilichojaa kahawa isiyo na sukari. Sekunde ishirini na nne zilitosha. Ujumbe ule tayari ulikuwa katika karatasi ile. Akaichana na kuitupia macho huku akivuta hatua kuielekea meza kubwa iliyowekwa kando ya nyumba ile, sambamba na dirisha lililoelekea barabarani. Kwa nje, wigo mrefu wa michongoma uliificha nyumba ile karibu robo tatu yake kutoka chini. Ni paa chakavu, lenye kutu na lililoliwa na hewa ya chumvi ndilo lililonekana kiurahisi.

Brian Mkuchu, aliketi kitini na kuiweka karatasi ile mezani. Mara baada ya kupiga funda moja la kahawa, akakitua kikombe na kuivuta ile karatasi karibu na uso wake.


Tafuta mzigo wenye Code 005 Ukiupata, upoteze bila maswali.


Brian akarudia kusoma karatasi ile mara kadhaa.

“Code 005!” akajisemea kwa sauti ya chini huku akiiendea simu ya mezani iliyowekwa kando. Akabofya vinobu kadhaa na kuweka mkonga wake sikioni. Utulivu wa kusubiri amkio la upande wa pili, ukatamalaki.

“Sabini na tatu A nakupata…”

“…Tafuta code 005 haraka unipe jibu,” akamwambia mtu wa pili.

“ Copy”.

Brian akakata simu na kurudi kitini. Alipoinua kikombe cha kahawa, tayari ilikwishapoa. Akasonya na kukisogeza kando. Akarudia tena kuisoma ile nukushi mara kadha wa kadha hasione nini kimejificha ndani yake.

“Code 005!” akajisemea tena. Alipotupa macho nje ya dirisha akaliona gari la kizamani,

Mazda jekundu likiwa limeegeshwa nje tu ya baraza la nyumba hiyo. Brian akatikisa kichwa


akalikumbuka Mazda lile ambalo sasa halikuwa maridadi kama kale. Akiwa bado katika kulitazama, simu ile ile, ikaita, akaiendea na kuinyakua kwa shauku, akaiweka sikioni.

“Sabini na tatu A…” akaitikia.

“Tukutane Ndege Beach tupate bia kidogo!” sauti ya upande wa pili ikamwambia.

“Umesomeka,” Brian akamjibu. Haikumpa tabu kuitambua sauti ile. Haraka akatoka nje na kuingia kwenye lile Mazda. Akaketi na kuufunga mkanda. Akaliwasha mara kadhaa likagoma kuwaka.

“Aaaaaaa shiiit!” akajikuta akipiga kelele peke yake. Alipojaribu mara hii likawaka. Muungurumo wake mzito ulilitambulisha kuwa halikuwa la kawaida. Akalitoa pale lilipoegeshwa na kuliingiza barabarani. Safari ikaanza.

Nusu saa baadaye aliwasili eneo la miadi, Ndege Beach. Akateremka na kuvuta hatua kuelekea kwenye baa ndogo iliyojengwa katika ufukwe huo. Baada ya kuzipita meza kama mbili tatu hivi, akaifikia ile anayoitaka, ambayo mwenyeji wake alikuwa kaketi peke yake, huku mbele yake kukiwa na chupa ya soda. Brian akavuta kiti na kuketi, akaondoa miwani yake nyeusi usoni na kuitia katika mfuko wa shati huku akiacha sikio moja lining’inie nje yake.

“Brian,” akaita yule jamaa kwa sauti ya chini.

“Yes Mic,” Brian akajibu huku akijiweka sawa kusikia alichoitiwa, “umetambua?” akamtupia swali akitaka kujua hasa juu ya kazi aliyompa. Kazi ya kuitambua code 005.

“Jambo jingine kaka, hatari…” akajifikicha jicho la kuume, kisha akaendelea, “faili limetoweka…” Mic akasema.

“What?” Brian akahisi kizunguzungu cha ghafla akajiegemeza kitini na kushusha pumzi ndefu, “Umejuaje?”

“Kama kawaida yangu, niliingia ofisini late sana, ukizingatia kamvua haka. Nafika kwenye shelf kwa minajiri ya kulichukua ili nianze ile kazi, silioni kaka…”

“Mike, Mike, Mike…” Brian akaita kwa sauti ya chini iliyojaa msisitizo huku akimkazia macho, “Kila mara nimekwambia; chunga hilo faili kwa sababu lina taarifa muhimu na tutazihitaji. Ona sasa, hata aliyechukua humjui… we are in trouble my friend,” akamwambia kwa sauti ya kukata tamaa.

“Unajua Brian, ile ni ofisi ya siri sana, haijulikani na watu… lakini ninachoshangaa, huyu mwanamke aliyeingia humu kaijuaje?” Mic akasema huku akitoa picha tatu; moja ikimwonesha Madam S akiwa ameingia mlangoni, ilimwonesha vizuri usoni. Ya pili ilimwonesha akiwa anachomoa kabrasha lile, na ya tatu alipoinama kuokota picha aliyoiangusha.

Brian alizichukua zile picha na kuzitazama kwa tuo, akamwangalia tena Mike.

“Ina maana humjui huyu mama? Na kama ameingia kwenye hii ofisi unayoiita wewe ‘ya siri’ basi ni mmoja wenu,” akamwambia.

“Simfahamu kabisa,” Mike akamweleza Brian.

“Ok, naondoka na hizi picha, naomba tuonane saa kumi na mbili jioni ukiwa na ile kazi yangu na mi nikiwa na majibu ya hizi picha,” Brian akamwambia Mike huku akiwa tayari keshasimama. Wawili hao wakaagana na kila mmoja akashika njia yake.



* * *



Mburahati NH


Nyumba aliyoinunua marehemu Dastan na kuikarabati tayari kuishi na mkewe Egra, ilikuwa Mburahati katika mtaa wa National Housing. Ilikuwa Imepita miaka takribani kumi hivi tangu kijana huyu atoweke. Ndugu na majirani hawakuweza kusema kwamba kafa , kwa sababu hawakuwa na ushahidi. Hivyo neno zuri lilikuwa ‘katoweka’. Kwa sasa nyumba hiyo ilikuwa imepangishwa.

Inspekta Simbeye aliegesha gari lake nyumba ya tano kutoka hiyo, akateremka. Upande wa pili, Madam S naye akateremka. Wote wawili, wakaikabili nyumba moja iliyokuwa mkabala nao. Simbeye, aliyevalia nguo za nyumbani; shati la Bahama na suruari ya kitambaa alikuwa wa kwanza kuzifikia ngazi hizo. Madam S alifuatia kufika hapo, akiwa hatua chache tu kutoka kwa Simbeye. Kama ungewaona, basi bila shaka ungejua kuwa ni mtu na mke wake. Kumbe walikuwa kazini.

Kabla awajaufikia mlango wa nyumba hiyo, ukafunguliwa. Mwanamama mmoja wa makamo akajitokeza. Wakakutana hapo kwa sadfa tu, kila mmoja akasimama na kuacha mita moja hhivi katikati yao.

“Habari yako dada!” Simbeye alikuwa wa kwanza kumsabahi. Umri wao haukupishana sana, ndiyo maana akamsabahi kwa kumwita ‘dada’.

“Salama tu. Karibuni sana…” yule mwanamke akawajibu huku akiifunga kanga yake vizuri.

“Samahani, hapa ndiyo kwa Bwana Kihwelo?” Simbeye akauliza. Yule mwanamke akabaki na butwaa. Hakujua nini anapaswa kukijibu. Baada ya sekunde kama tano hivi akawajibu.

“Kihwelo! Kihwelo yupi? Maana anayeishi hapa anaitwa Chami. Amepanga nyumba hii yote…” akaeleza.

“Ok! Samahani tutakuwa tumekosea, maana tunauliza tangu hukoooo tukaelekezwa hapa. Tuna muda mrefu sana hatujaonana,” Simbeye akasema.

“Ni ndugu yangu ndiyo. Ni miaka kama thelathini hivi tangu tuachane na kiukweli hatukuwa na mawasiliano.” Simbeye akatunga uongo.

“Oh poleni sana, hapa tumehamia miaka sita iliyopita na kwa kweli, simjui mtu huyo, labda uliza kwa majirani au mjumbe nyumbani kwake paleeee,” akawajibu na kuwaonesha kwa kidole nyumba ya Mjumbe wa eneo hilo.

“Asante sana!” Simbeye akajibu. Simbeye na Madam S wakatembea taratibu mpaka kwenye nyumba ya mjumbe. Bahati nzuri wakamkuta kibarazani akicheza bao na wazee wenzake.

Walipojitambulisha kama ndugu wa bwana Kihwelo, yule mzee akawakaribisha ndani na kuketi sebuleni.

“Mnasema ninyi ni ndugu wa Kihwelo?” akawauliza.

“Ndiyo! Na hatujaonana na huyu bwana miaka mingi sana. Na hii inatokana na kwamba hatukuwa na ukaribu sana kimawasiliano…” Simeye akajibu wakati Madam S akiwa kimya kabisa.

“Mh! Mmmmh!”

“Vipi mzee wangu mbona unaguna?” Simbeye akauliza swali.

“Nashindwa nianzie wapi…”

“Usijali mzee, sisi twahitaji kujua ndugu yetu yuko wapi. Laiti tungekuwa na ndugu hapa Dar’ ingekuwa rahisi,” Simbeye akaeleza.

“Mzee mwenzangu! Hapa habari wala si nzuri,” aliposema hayo, Madam S akarudisha macho kwa yule mzee, “Kihwelo bwana, dah! Huyo kijana bwana aaa alitoweka tu katika mazingira ya kutatanisha yeyena mkewe, tena siku ya ndoa yao!” yule mjumbe akeleza kwa kigugumizi kidogo, akatulia. Simbeye na Madam S wakamkodolea macho ya mshangao uliochanganyika na majonzi kwa wakati mmoja.

“Na alikuwa akiishi wapi?” Simbeye akamuuliza.

“Huyu bwana, nyumba yake ilikuwa ile pale, na sasa wameipangisha,” mjumbe akajibu.

“Ok, sawa, tutafanyaje sasa… mi nitaendelea kuwatafuta ndugu wengine huko Iringa ili nipate habari kamaili,” Simbeye akasema huku akionekana wazi kuwa anataka kuaga. Dakika kumi zilizofuata, Simbeye na Madam S walikuwa tayari ndani ya gari lao.

Mpango huu ni kigae katika choo changu cha ndani. Madam S akawaza. Moja ya sentensi

iliyoandikwa katika ule ujumbe wa siri.

“Inabidi vijana warudi baadae kuipekuwa ile nyumba,” Simbeye akasema. Madam S akashusha pumzi na kumtazama mzee huyo.

“Hilo niachie mimi, kesho asubuhi nitakupa habari,” Madam S akamwambia Simbeye.




Mpango huu ni kigae katika choo changu cha ndani. Madam S akawaza. Moja ya sentensi

iliyoandikwa katika ule ujumbe wa siri.

“Inabidi vijana warudi baadae kuipekuwa ile nyumba,” Simbeye akasema. Madam S akashusha pumzi na kumtazama mzee huyo.

“Hilo niachie mimi, kesho asubuhi nitakupa habari,” Madam S akamwambia Simbeye.


* * *


2:35 usiku


MWINYIJUMA SOCIAL HALL


Mwananyamala


Muziki wa bendi ya Vijana Jazz uliendelea kuunguruma ndani ya ukumbi huo mkongwe jijini Dar es salaam. Mmoja kati ya wapenzi wa bendi hiyo aliyekuwa katikati ya umati akilisakata rumba alikuwa Kamanda Amata. Hakuwa na hili wala lile, binti aliyekuwa naye alikuwa hodari pia katika hilo. Alijua kulisakata ‘Air Pambamoto’, alimpagawisha Amata kwa mauno aliyokuwa akiyazungusha. Hata wanaume wengine pembeni yake, walijikuta wakiacha kucheza na kuwatazama wawili hawa.

Honi za gari zilizopigwa nje ya ukumbi huo zikamgutusha kutoka katika lindi la burudani. Honi zile zikarudia tena. Na mara ya tatu ilipopigwa tena, Amata akamshika mkono yule mwaDanada na kutoka naye kwenye kundi lile la watu.

“Aaaaaaa mrudisheee, mwacheeee!” kelele za wanaume walionogewa na unenguaji wake zikasikika. Amata hakujali, akamvuta mkono mpaka katika mlango wa kutokea nje. Akamwacha , kisha yeye akavuta hatua kama tano mbele, karibu kabisa na barabara. Akasimama na kuangaza huku na kule.

‘Piiiiii! Piiii! Pi!’ honi ikasikika tena, mara hii kwa mtindo mwingine. Mara moja akaliona gari lililokuwa likipigwa honi hizo. Alipotaka kuvuka barabara, akashikwa mkono.

“Mbona unataka kunitoroka?” yule msichana alikuwa pembeni mwa Amata akihoji.

“Oooh, tangu lini nikamwacha mrembo kama wewe? Nilitaka nimwone rafiki yangu pale ng’ambo kisha tuendelee na burudani zetu,” Amata akamjibu.

“Mmmmm!”

“Mmmmm nini?” Amata akauliza.

“Wanaume wote baba yenu mmoja. Maneno matamu kinywani lakini hisia hakuna moyoni,” yule msichana akalalama huku kaibetua midomo yake kama anamsuta mtu. Kamanda Amata akavuka barabara na kumvuta yule msichana mpaka upande wa pili.

“Eh, baba utaniangusha! Polepole,” akamwambia Amata. Hakumsikiliza. Akavuta hatua mpaka kwenye lile gari. Alipolikaribia tu, kioo cha mbele kikateremka nusu.

“Vipi?” Amata akamuuliza dereva wa gari hiyo.

“Twende!” Chiba akajibu. Amata hakuuliza tena, akafungua mlango na kumkamata yule msichana, akamnyayua na kumuweka kwenye siti ya nyuma, naye akapanda na kuketi kandoye.

“Mnanipeleka wapi jamani?”

“WE tulia, shida yako nini!” Amata akamtuliza yule mwanamke.

“Vipi Chiba?” akamuuliza.

“Ondo!” Chiba akajibu akimaanisha ‘Ofisi Ndogo’.

“Ok, pita Virginia kwanza,” Amata akamwelekeza Chiba. Naye akatii. Akaiacha barabara ya Kinondoni kuelekea daraja la Salender na kuingia mtaa wa vumbi na mashimo upande wa kulia. Dakika mbili tu ziliwafikisha Virginia.

“Adella, nitakukuta hapa lodge, naenda kucheki kitu Fulani , ninakuja…” Amata akasema.

“Utarudi kweli wewe? Au ndo umekatisha starehe zangu tu?” Adella akauliza kwa mashaka. “Nitarudi, fika mapokezi mwone Lilian!” akamwambia huku tayari msichana yule akiwa chini. Hatua zake za maringo zikamfanya Amata asahau kurudi garini. Alikuwa mfupi, mnene, nywele zake zikiwa katika mtindo wa Afro. Sketi fupi aliyovaa ilitosha kudhihirisha uzuri na utamu wa mguu wake mnene, mapaja yaliyojaa vyema, kiuno kidogo kilichobeba kiwiliwili chenye afya.

“Hivi hizi mbegu unazitoaga wapi?” Chiba akauliza. Amata hakujibu, badala yake akaingia garini na kuketi siti ya mbele. Akamtazama Chiba na kuanza kucheka.

“Nambie Chiba!”

“Bibi yako anakutafuta huko!”

“Nipeleke nikamwone tafadhali,” akamwambia Chiba.

* * *


Ofisi ndogo


Madam S alikuwa kimya ofisini kwake usiku huo. Mbele yake, juu ya meza kulikuwa na kitabu chake cha kumbukumbu, kikiwa wazi. Miwani yake ikiwa imetulia juu ya kurasa hizo zilizo wazi. Akiwa kazama katika lindi la mawazo, sauti hafifu ya kengele ikamgutusha. Alipotazama luninga yake ndogo iliyowekwa mahali pa siri katika meza yake hiyo. Akawaona vijana wake wawili wakiwa mita chache tu kabla ya mlango. Akabofya kitufe katika uvungu wa meza hiyo. Mlango ule ukafunguka na kuwaruhusu kuingia ndani.

“Karibuni, ketini tafadhali,” akawakaribisha na kila mmoja akaketi katika kiti chake. Ndani ya ofisi hii palikuwa na viti sita tu. Kwenye meza zilizofanya T palikuwa na kiti kimoja upande wa mbele na vitano vilikuwa upande mwingine. Viti vyote hivi vilikuwa nadhifu sana, kila kimoja kikiwa na namba na nembo safi ya TSA. Amata na Chiba wakaketi wakimtazama HOT.

“Giza limeingia, usiku umetamalaki… kazi inayotukabili bado ni kitendawili. Nyote mnajua.

Sasa naitaji ifanyike blackbag job usiku huu. Nitakaa hapa hapa nikiwasubiri,” Madam S akawaambia. Amata na Chiba wakatazamana, kisha wakarudisha macho kwa mwanamama huyo.

“Wapi?” Amata akauliza. Badala ya kujibu, mwanamama huyo, mkuu wa idara nyeti ya kijasusi, akamsogezea kijana wake karatasi moja nyeupe iliyo na maandishi machache tu.


Wamesema wakimgundua mamluki yeyote anayekwamisha juhudi zao watamuua bila huruma.


Ni mimi si mwingine, wataniua, lakini lazima niufikishe mpango huu dhalimu mikononi mwa serikali.


Mpango huu ni kigae katika choo changu cha ndani.


Na mengine mengi niliyoyakosa yapo katika nyumba namba 73A Kinondoni Mtaa wa

Galu. Nyumba hii ni mali ya Burushi mmoja mwenye urafiki wa karibu sana na

Kibwana Mtokambali… Dastan Kihwelo


Ni ujumbe uleule ambao Madam S aliukuta katika kabrasha lile. Amata akausoma na alipomaliza akampatia Chiba, naye akausoma.

“Nipe mwongozo mkuu …” Amata akamwambia Madam S huku akijiweka vizuri kitini.

“Maandishi hayo, au niite ujumbe huo umeandikwa na marehemu Dastan Kiwelo. Huyu alikuwa mwanausalama katika idara yetu miaka hiyo ya tisini. Hatujua kama aliuawa au emetekwa na kufichwa mahali Fulani. Hatujui, lakini alitoweka mara tu baada ya harusi yake yeye pamoja na mkewe. Tukio hilo lilitukia mwaka tisini na moja,” Madam akaeleza kwa kifupi.

“Dastan Kihwelo! Sasa blackbag hii inahusiana na nini hasa?” Amata akauliza.

“Swali zuri ila kitoto kuulizwa na mtu kama wewe…”

“Najua…”

“Dastan Kihwelo, alikuwa akifanya kazi kama D.A. Mkuu wake wa kazi kipindi hicho alimruhusu kurubuniwa na kujiuna na kundi la wanamapinduzi waliokuwa wakifanya mambo yao kwa siri sana hapa nchini. Kundi hili liliundwa mara baada ya sakata la kujaribu kuiangusha serikali ya awamu ya kwanza mwaka ule wa themanini na mbili, uliopelekea wengine kufungwa na wengine kutoroka nchi. Hili mnalijua!” akawaeleza.

Amata na Chiba wakatikisa vichwa vyao kuonesha kuwa wanalifahamu vyema. Sifa moja wapo ya mwanausalama katika idara hizi za kijasusi ni kujua historia ya nchi yako, mahali unapoishi na watu wanaokuzunguka. Madam S akaendelea kuwaambia, “Sasa huyu kijana aliweza kupata habari nyingi sana. Mojawapo ndiyo iliyofanikisha sisi kummaliza Mwakibinga, mpo?”

“Tupo!”

“Hivyo basi, katika kutoka pale tulipokwama, nimeipata memo hiyo hapo. Na katika kuichambua kitaalam utagundua kuna maeneo mawili yametajwa. Moja limetajwa wazi kuwa ni ‘nyumba namba 73A Kinondoni Mtaa wa Galu’, na nyingine ameitaja kwa fumbo kwa maneno ‘Mpango huu ni kigae katika choo changu cha ndani’” akawaeleza.

“Kwa hiyo hicho kigae kina mengi!” Amata akasema.

“Yes!”

“Kazi imekwisha,” akamhakikishia mkuu wake akiwa tayari wima.

“Sasa unasimama unajua unaenda wapi?” Madam S akamuuliza Amata ambaye tayari alikuwa

wima.

“Si umeshatuambia ‘ni kigae katika choo changu cha ndani’ au?” akauliza.

“Ndiyo. Mburahati, National Housing, kitalu namba 21B. Nawasubiri hapa hapa…” Madam S akawaamuru. Amata na Chiba wakatoka katika ile ofisi na kuliendea lile gari. Wakaingia na kuketi ndani yake.

Amata akashusha pumzi ndefu, akavuta mkanda wa usalama na kuupachika vyema katika

bako yake. Chiba na Amata, usiku huu walikabiliwa na kazi hiyo ‘blackbag’ yaani uchunuzi ama wa nyumba au ofisi hasa katika nyakati za usiku. Haikuwa kazi kwao kuvamia nyumba isiyo na ulinzi kama hiyo. Wakatazamana, kila mmoja akaelekeza macho yake mbele.

“Twende Kinondoni, nyumbani, tukaandae vifaa kisha usiku wa saa nane tuifanye kazi hiyo,” Amata akamwambia Chiba. Chiba, badala ya kujibu, akaitazama saa yake. Saa tano kasoro usiku.

“Halafu tunapoisubiri saa nane tutakuwa wapi?” Chiba akamtupia swali Amata. Sekunde

kadhaa zikapita bila neno. Ukimya ukatamalaki kati yao.

“Utaniacha kwa Adella, pale Virginia Lodge. Au umesahau kama nimeacha mtoto pale?” Amata akamwambia Chiba, wakati huo tayari ari likiwa juu ya barabara ya Mtaa wa Shaban Robert.

Safari ya Kinondoni.

“Sawa kaka. Ila angalia pia na upande wa pili. Gina anakupenda sana ila umtendei haki…” Chiba akamwambia Amata.

“Chiba, ya Gina yaache. Twende home tucukue vifaa, uje uniache kwa Adella wangu,” Amata

akasisitiza.





MBURAHATI


Saa 8:15


Kamanda Amata aliegesha gari mbele ya maduka, mitaa mitatu kabla ya ule waliolekezwa. Walipohakikisha milango yote imefungwa, wakavuta hatua kuilekea nyumba waitakayo. Usiku wa manane, wakiwa ndani ya mavazi meusi, Chiba na Amata waliikaribia kabisa nyumba waitakayo. Ukimya ulitamalaki, walichukua dakika moja kuizunguka nyumba hiyo. Hakuna aliyekuwa akiongea kwa sauti, lugha ya viziwi ilikuwa ikitumika. Walipohakikisha kila kitu kipo sawa, wakauendea mlango wa mbele. Wakapeana ishara, Chiba akapachika funguo na kuzungusha. Mlango ukaitikia. Chiba akausukuma taratibu na kukaribishwa na korido ndefu iliyogawanya vyumba upande huu na ule. Wakapeana tena ishara nyingine. Amata akachomoa makopo matatu ya dawa aina ya Chlorofom yenye ujazo wa mililita mia tano kila moja. Akampa ishara Chiba, kila mmoja akavaa barakoa maalumu ya kuzuia aina yoyote ya gesi kutomdhuru mtumiaji. Akaondoa kifungo cha chupa moja na kuisukumia koridoni huku ikitoa kitu kama majimaji mepesi yakisindikizwa na harufu nzuri. Wakaingia ndani na kufungua kila chumba wakinyunyiza kiasi kidogo cha kuwafanya wenyeji walale kwa saa mbili tu.

Dakika tano zilitosha kuwalaza wote mle ndani. Chumba cha mwisho kabisa ndicho hasa walikuwa wakitakacho. Jinsi kilivyojengwa kilionekana wazi kuwa kingekuwa cha mwenye nyumba. Kilikuwa kikubwa kilichowekwa makochi matatu ya kisasa. Luninga moja ya Hitach na redio kubwa ya Panasonic Double Deck. Upande mmoja kulikuwa na mlango. Amata akahisi kwa vyovyote kitakuwa chumba cha kulala. Akampa ishara Chiba naye akakifuata mpaka mlangoni. Akajaribu kuufungua mlango, ukagoma. Akatumbukiza funguo yake isiyoshindwa, akanyonga mara moja tu. Kitasa kikatii. Akausukuma mlango taratibu na kukaribishwa na watu wawili waliokuwa kitandani wakikoroma. Mwanamke na mwanaume, pembeni ya kitanda kulikuwa na meza ndogo iliyobeba chupa kubwa ya Amarula na pakiti sita za mipira ya Salama.

Amata akampa ishara Chiba ya kuingia ndani ya chumba kile, naye akafanya hivyo na kumuelekeza moja kwa moja kwenye mlango wa chooni kwa kuwa chumba hiki kilikuwa ni self container. Amata akawatazama wale viumbe pale kitandani waliokuwa usingizini bila nguo huku suka likiwa limesongwasongwa kando ya kitanda. Feni lilikuwa likiunguruma na kujaribu kupambana na joto la jiji hilo lakini wapi. Amata akapuliza tena dawa ile karibu nusu kopo kwa kuwa watu wale walikuwa wamekunywa pombe.

* * *

Hakikuwa chumba kikubwa. Sinki la choo cha kukaa na kipande kingine kulikuwa na pazia la plastiki kutenganisha maeneo mawili hayo nyeti. Kamanda Amata akachukua ufagio na kutumia mpiniwe kugongagonga vigae vya sakafu kuona kama kuna yoyote ambayo itaonesha dalili za shimo. Kwa kusikiliza mlio uliokuwa ukisikika, Chiba akaaundua kiurahisi zaidi. Akamwonesha kwa kidole kigae alicho na wasiowasi nacho. Vyote vilitoa mlio sawa wenye tofauti ndogo sana. Ilihitajika masikio makini sana. Bila kuchelewa, Amata akashusha begi lake na kuchukua mashine ndogo ya kukata vigae. Akakiwasha na kukata sawasawa na miungo ya vigae hivyo. Alipofanikiwa akachukua kifaa kingine na kubandua vigae vile. Chini ya kigae kimojawapo kulikuwa na mfuniko mdogo wa mbao. Akaukamata na kuutoa. Chini kulikuwa na mfuko wa plastiki uliofungwa vyema kabisa. Amata akautazama kwa kusaidiwa na kurunzi ndogo iliyokuwa katika paji lake la uso. Akauvuta taratibu na kuutoa, akauweka sakafuni. Ndani ya mfuko ule kulikuwa na bahasha moja ya kaki, iliyofungwa na kugongwa mhuri wa ‘SIRI’. Akampa ishara Chiba kuwa waufungue, naye akajibu kwa kumwambia kuwa wataufunua ofisini.

Kazi ikaisha, Amata akarudisha vile vigae kama vilivyokuwa. Kwa kutumia gundi maalumu akavibandika kiasi kwamba si rahisi kugundua kuwa vilifumuliwa. Wakapakia kila kitu kwenye mkoba wao. Amata akauweka mgongoni na kutoka mpaka pale chumbani. Mtu na bwana wake walikuwa wamelala fofofo. Kila mmoja katupa mguu anapopajua yeye na kuacha siri zote nje.

Joto la Dar’ halina adabu! Amata akawaza. Haraka akauendea mlango, Chiba alikuwa tayari sebuleni. Amata alipoufikia mlango, akasita, akageuka nyuma na kutupa jicho juu ya meza ndogo ya urembo. Macho yake yakaiona pochi ya kike. Akarudi kuifuata na kumwacha Chiba akiwa hajui kinachoendelea. Akaufungua ule mkoba na kupitisha macho kijasusi, vidole vyake viwili yaani kile cha shahada na kati vikapenya na kuchomoa kadikazi, akaitia mfukoni. Alipotaka kutoka, akasita, akamtazama yule bwana pale kitandani. Akili yake haikumpa jibu sahihi, vinyweleo vikamsimama. Akainua mkono na kumpa ishara Chiba. Ishara ya hatari. Kutoka sebuleni, Chiba akachomoa bastola yake ndogo, akapachika kitu kama sindano kwenye mtutu wake. Akaiweka tayari. Kwa kutumia saa yake ya kisasa, Amata akampiga picha yule jamaa. Ni sekunde ileile alipojikuta akitazamana na mtutu wa bastola kutoka kitandani.

“Nilikuwa nakusubiri kwa hamu sana mjinga wewe,” yule jamaa akamwambia Amata, “Lete mlichokichukua!” akang’aka. Amata hakuwa na ujanja kwani domo la Magnum 22 lilikuwa likimtazama kwa uchu. Akataka kuingiza mkno kwenye jaketi lake ili atoa ile bahasha.

“Acha! Weka mikoni yako juu,” yule jamaa akamwamuru Amata huku akiteremka kitandani uchi wa mnyama, “Ninachukua mwenyewe, na ukileta kokolo kuna bastola tatu zinakutazama, zote zitakuchakaza kabisa”. Akamwambia kisha akapachika mkono kuitoa ile bahasha. Chiba hakifanya makosa, akafyatua ile bastola kutoka mafichoni. Kile kisindano kikapaa kwa shabaha malidhawa na kutua shingoni mwa yule jamaa. Yule bwana akatulia kama sekunde tatu hivi, akakichomoa na kumtazama Amata. Macho yake yalikuwa yakirembua kama mwenye usingizi mwingi. Konde moja zito sana kutoka kwa Kamanda likamshukia na kumbwaga chini. Amata akakiendea kile kitanda. Akavuta shuka na kulitupia huko. Kamera ndogo ikaanguka chini akaiokota.

“Mh!” akaguna. Akaitazama saa yake, ilikuwa tayari saa tisa na kitu. Akachomo kifaa chake kingine cha kumwezesha kutambua camera za siri. Akaangaza kila kona, kwenye maua ya urembo, taa ya juu, feni, na kila kona, hakuna kamera.

Haiwezekani! Akawaza. Akazichunguza picha za ukutani, alipoifikia picha ya Monalisa, kile kifaa kikatoa mwanga mwekundu. Akaiende na kuitoa palle ukutani, akakutana na kamera ndogo iliyofungwa kiufundi sana. Akaichomoa na kuitia mfukoni. Kamera nyingine akaikuta nyuma ya kioo cha meza ya urembo. Akaichukua. Alipojiridhisha kuwa kila kitu kipo sawa, wakatokomea zao nje ya nyumba hiyo.

Kwa hatua za haraka haraka wakakata mitaa mpaka walipoliacha gari lao. Wakaingia na kuketi. Chiba upande huu na Amata nyuma ya usukani. Akatia injini moto na kutoka katika ile barabara kuitafuta ile ielekeayo Kigogo. Kwa mwendo wa wastani wakakiacha kitongoji hicho na kuikamata Manzese, wakatokea Barabara ya Morogoro na kutokomea mjini.



WAKIWA KATIKA maficho yao, Mc Tee, Big J na Bi Jesca waliagana wakiwa bado hawajapata ufafanuzi way ale wayatakayo. Walifikia muafaka wa kurudi kila mmoja anakoishi na wasubiri taarifa moja tu kutoka kwa Mc Tee. Kila mmoja alitumia njia yake ya siri kuondoka katika kisiwa hicho. Mc Tee baada ya kuagana na wenzi wake, alirudi ndani na kujitupa kochini. Akaminya kitufe Fulani chini ya meza yake. Sekunde chache tu, yule mwaDanada mrembo akaingia tena katika sebule ile nadhifu. Hakuwa mwingine, Hassna.

“Sikiliza Hassna, ni wewe pekee unayeingia katika chumba hiki. Narudia tena kwako, unachokiona humu kiache humuhumu. Wanaokuja humu wala usiwaulize wanatokea wapi. Ukikaidi, utakufa…” Mc Tee akamuaonya msichana huyo.

“Sawa bwana, kila siku nakuahakikishia kuwa ninakuelewa na siwezi kukaidi maagizo yako,” Hasna akajibu kwa unyenyekevu huku mikono yake kaikutanisha viganja mbele, chini kidogo ya tumbo lake.

Mc Tee alirudi kwenye meza yake ya kompyuta akimwacha msichana yule akitoka na kuingia chumba kingine. Alipohakikisha hayupo, akawasha kompyuta ile na kuunganisha kamera zake za usalama zote. Akachunguza kila kona ya kambi yake kuanzia nyumbani kwake mpaka kwenye hoteli kubwa na ile sehemu iliyojengwa apartment za wageni. Akaingia kila chumba kwa kutumia kameara za siri zilizofungwa katika vyumba hivyo. Akashuhudia yote ya chumbani nay a sebuleni ambayo wageni wake walikuwa wakiyafanya. Akatazama chumba cha mikutano na kusikiliza kila alichotaka na kile alichokuwa na wasiwasi nacho akakiandika kwenye kitabu chake cha kumbukumbu.

Akawatazama wageni wake mpaka walipopotelea kwtika upeo wa macho yake na kubadilika kuwa watalii katika kisiwa hicho. Akiwa ametingwa na kucheza na kamera hizo, simu yake ya mezani ikaita kuashiria nukushi iliyokuwa ikisubiri kuruhusiwa. Akaijibu kwa kuiruhusu, nayo ikaanza kujichapa katika karatasi. Ilipomaliza, akaikata na kuiweka mezani. Ulikuwa ujumbe. Ujumbe mfupi tu lakini wenye ujazo mwingi.


Mshenzi ametuwahi,

hatukuwa tumejua wapi Dastan ameificha ile siri.

Mshenzi ameichukua tukiwa chumbani humohumo.

Tumeinasa picha yake, tumeituma kwako.

Mc Tee alijikuta anaingiwa na baridi kali, hakujua nini anapaswa kufanya. Mwili ukatetemeka kwa hasira, moyo ukadunda woga na nywele zikasimama kwa hatari inayomkabili. Ni kwa miaka mingi walikuwa wakiitafuta siri ambayo Dastan aliificha baada ya kuichukua kwenye mikono ya Bambros. Siri nzito, iliyobeba kila baya kwa serikali na jema kwao. Mikakati, misaada, wahusika na kila kitu kilikuwa humo. Ni siri hii iliyofanya Dastan auawe. Aliikumbati, akaificha kisha maelekezo akayaweka katikaofisi nyeti na ya siri ya Chameleone kule Ocean Road. Pamoja na kupata pandikizi jingine ndani ya serikali, bado walishindwa kujua wapi siri ile ilifichwa. Wakafanya kila njia, wakaiweka mkononi nyumba ya Dastan ilikuona kama kuna chochote kitatukia.

Mc Tee akaigeukia kompyuta yake, ndani ya barua pepe akaipata picha aliyotumiwa. Mtu aliyevaa barakoa ya kuzuia hewa ya sumu. Hakuitazama sana, akaituma kwa rafiki yake Zelda akiomba msaada wa utambuzi wa kiumbe huyo. Alipojiridhisha kuwa imekwenda , akajitupa kitini, akaweka mikono kichwani huku macho akiyakodoa kuitazama picha ya Rais iliyokuwa ikininginia ukutani.

You are dead, Bastard! Akawaza, akiiambia ile picha. Lakini cha kushangaza, ile taswira ndani ya picha ilikuwa ikitabasamu daima kila ikimwangalia.

* * *

SIKU TATU BAADAE


SHAMBA


Kamanda Amata na Madam S walikutana katika chumba cha siri ndani ya jengo hilo. Kikao hicho cha wawili kiliitishwa na mwanamama huyo mara tu baada ya kukamilisha uchunguzi wa tafutishi ile waliyoipata katika nyumba ya Dastan.

“Unajua mpaka sasa hatujui nini kimempata Dastan…” Madam akamwambia Amata na kuiweka miwani yake vizuri, “…si yeye tu, hata mkewe,” akamalizia kusema.

“Miaka yote hii Madam, watakuwa washamuua,”

“Na kilichomuua ni hiki,” akamwambia akimaanisha ile bahasha, “Kama angekuwa hai, huyu kijana angekuwa katika ofisi hii,” akasema.

“Pole!”

“Asante,” akatulia kidogo na kushusha pumzi, “Sasa kuna kazi hapa Amata, inabidi uingie mzigoni. Tumeshapata pa kuanzia ili kuwamalizia hawa wawili waliyobaki yaani Kibwana Mtokambali na James Msambamagoya. Kama Dastan alivyodokeza kuwa ‘mkakati huu ni wa kudumu mpaka chama tawala kitoke madarakani iwe kwa damu au kwa maji’. Kwa maana hiyo lazima hukumu yao itekelezwe kama Jaji Mzava alivyohitimisha,” Madam akamwambia TSA 1 aliyekuwa mbele yake.

“Nakusikiliza HOT…”

“Kuna hii picha hapa ya huyu mwanamke, sijui ni mzungu au mwarabu, mtazame vizuri,”

“Kwani Chiba hakumtambua?”

Badala ya kumjibu, Madam S akamsogezea karatasi nyingine. Amata akaipokea, akaitazama juu yake na kuona picha ya yule mwana mke na maelezo kadhaa chini yake. Maelezo yale yalimtambulisha kwa jina la Babier Saratov, raia wa Jumuia ya Kisoviet ya Urusi ambayo mpaka wakati huu ilikuwa imesambaratika.

“Anaitwa Babier, yupo Saratov, Rusia,” Madam akamwambi.

“Kwa hiyo inabidi nifike Saratov?”

“Ikibidi dear…”

“Sawa Madam, ila naomba saa ishirini nan ne kuna kazi ndogo niimalize, kisha nitakuwa tayari kwenda popote utakapo isipokuwa kuzimu…” Amata akasema na kutia utani wake kama kawaida.

“Sawa, nakuhitaji hapa kesho kama saa hizi, tiketi yako itakuwa ta…,” Madam akakatishhwa na simu iliyoita kwa fujo. Akaichukua.

“Hello!” akaita.

“Wizara ya mambo ya nje inaongea,” sautiya upane wa pili ikajibu.

“Kwa niaba ya ofisi Alfa, Mambo ya nje unasomeka,” Madam akajibu kwa utambulisho huo. “Mwanausalama Dana Kalangila kutoka Lisbon atatua leo na ndege ya shirika la Swizz saa nne kamili

usiku. Ana mzigo wenu pokeeni tafadhali,”

“Copy!”

“Over and Out”

“Out!” Madam akakata simu. Akamtazama Amata usoni.

“Vipi?” Amata akauliza.

“Kumekucha mwanaume. Dana anaingia usiku huu saa nne na Swizz…” Madam akamwambia Amata.

“Habari nzuri hiyo, Gina na Jasmin watashughulika naye…” Amata akajibu.

Baada ya kupanga mikakati na kuiweka sawa, Madam S na Amata wakaagana kwa miadi ya kukutana muda wowote kabla ya hizo saa ishirini na nne kutimia kama ikibidi.

* * *

Kamanda Amata aliegesha gari jirani kabisa na maduka ya vifaa vya ofisini mbele ya chuo cha uandishi wa habari DSJ. Kutoka katika mfuko wake wa Suruali, akachomoa kadi kazi ile aliyoichukua katika kile chumba usiku uliopita.

“Mariam Shemweta,” akasoma jina na kutamka kwa sauti ya chini. Kwenye ile kadi kazi alipata jina na namba ya simu. Kadi ile ilimwelezea Mariamu kuwa ni mkufunzi katika chuo hicho. Hii haikumsumbua Amata kufika eneo hilo tayari kufanya kile anachokitaka. Taswira ya mwaDanada huyo akiwa kitandani usiku uliopita ilimjia Amata, akameza mate. Akachukua simu yake na kupiga namba Fulani iliyokwenda moja kwa moja injinia wa kampuni ya simu.

“Ndiyo kaka nambie!” sauti ya upande wa pili ikajibu.

“Swedi, kama kawaida…”

“Wapi leo nipe codes nifanye kazi,” Swedi akamwambia Amata.

“Nataka unifanyie Carnivore…”

“Lete codes!” Swedi alimwambia Amata. Alishaelewa lugha hiyo ya kijasusi ‘Carnivore’ ikimaanisha kuingilia mawasiliano ya mtu. Swedi, injinia wa simu katika mtandao wa DarCom aliipokea namba ya Mariamu kutoka kwa Amata na kuiingiza katika kompyuta yake. Kwa kutumia njia za kielektroniki akaiunganisha simu ya mwanamke huyo na ile ya Amata.

“Hey man!” akamwita Amatya ambaye alikuwa bdo yupo hewani.

“Yes!”

“Kazi imeisha, wash simu yako ile ya akiba, alafu iache wazi muda wote. Ili upate mawasiliano hayo vizuri, basi tumia blutooth device kaka,” akamwambia.

“Sawa nimekupata,” akamjibu.

“All the best, ukimaliza unipe tone nifunge. Angalia tu usije kuua mtu maana we na hao viumbe, nahisi ushahisi unaibiwa…. Hah hah hah hah” Swedi akamwambia na kumtania.

“Aaaaa ha ha ha … hamna bwana, Man at work!” Amata akamjibu na kuangua kicheko.

“Ok, ova!”

“Ova”.

Kmanda Amata, akawasha ile simu aliyoambiwa na kupachika kwenye dashboard ya gari. Akaingiza tarakimu nne za siri na kuifanya simu ile iwe hewani muda wote. Hivyo mawasiliano yote yanayotokana kuingia kwenye simu ya Mariamu yalisikika hapo bila shida. Akachukua kifaa chake cha masikioni na kukipachika. Ungemuona ungesema ni kiziwi kutokana na kifaa kile kilichofanana kwa umbo.

Mara tu baada ya kupachika, akakuta tayari kulikuwa na simu hewani. Akasikiliza kwa muda na kucheka tu. Ilikuwa simu ya Mariamu akiongea na shoga yake. Mazungumzo yao yalijawa na umbea.

Wanawake bwana, wanaacha kufanya kazi wanapiga umbea! Akawaza huku akiendelea kuwasikiliza. Muda huohuo, mbele ya gari lake kukaegeshwa Jaguar jeupe. Hakuna mtu aliyeshuka. Wakati umbea ule unaendelea kwenye ile simu aliyokuwa akisikiliza Amata, akasikia simu nyingine ikiingia katikati yake.

“Shoga subiri naona hubby ananipigia, nitakucheki baadae,” Mariamu akamuaga shoga yake. Mara tu simu ile ikapokelewa.

“Yes dear nimekumiss… unaendeleaje?” Sauti ya Mariamu ikasikika.

“Niko poa, lakini naapa mbele ya Mungu nikimtia mkononi yule shetani nanyonga,” sauti ya kiume ikasikika.

“Kabisa yani, jizi lile, halafu limetuvamia usiku… mi majizi siyapendi…”

“Usijali, nimekufuata, nipo hapa nje…”

“Sawa mpenzi nakuja, ngoja nifunge ofisi kabisa,” sauti ya Mariamu ikamjibu yule mtu wa kwenye gari. Ile simu ikakatika. Kamanda Amata akacukua kamera yake ndogo na kuitega tayari kupata picha atakazo. Dakika kumi baadae, mwanamke mmoja mwenye mwili wa wastani akajitokeza getini na mkoba mikononi. Suti aliyovaa ilionesha haswa kuwa ni mkufunzi. Hijab , kichwani mwake ilimtambulisha vyema kuwa ni muumini wa dini gani. Badala ya kupiga picha, Amata akajikuta akimkodolea macho. Akamtazama kutaka kujua kama ni yeye au la.

Ni yeye! Akajisemea moyoni, akaweka tena kamera yake vizuri na kupata picha kadhaa. Mlango wa dereva wa lile Jaguar ukafunguliwa. Kijana mtanashati akateremka na kuzunguka upande wa abiria, akafungua mlango. Sekunde hiyohiyo, Mariam akafika, wakakumnbatiana, kisha akapanda garini. Yule kijana naye akarudi upande wake na kuingia. Taratibu lile gari likaanza kuyaacha maegesho na kuingia barabara ya Simple kurudi barabara kuu ya Uhuru. Kamanda Amata akaipachika kamera mahala pake na kuanza kuwafuata taratibu.

Lile gari likaikamata barabara ya Uhuru kuelekea Kariakoo. Kamanda Amata akiwa katika makutano ya barabara ya Amana na Uhuru, akasubiri maari matatu yakae katikati yake na yule anayemfuata. Kisha naye akaingia na kumfuata taratibu. Safari ilikuwa ndefu mpaka mitaa ya Mbuyuni, Oysterbay. Barabara ya kwanza, ya pili, lile Jaguar likakunja kona kulia na kuingia mtaa wa Galu. Amata naye akakunja kwa kuwa njia hiyo pia ingeweza kumfikisha nyumbani kwake. Mita kama mia mbili hivi lile jaguar likasimama getini, Amata akapitiliza na kuendelea mbele. Hakwenda mbali sana, akaegesha gari kwenye mgahawa mmoja kando tu. Akateremka. Akaichomoa ile simu kutoka kwenye dash board na kuitia katika mfuko wa shati. Akavuta hatua taratibu kurudi kule lilikoingia lile Jaguar. Geti la nyumba hiyo lilifungwa, lile gari lilionekana kwa ndani. Akavuta hatua na kuingia mtaa mwingine. Kwa sadfa tu akakuta fundi viatu na mng’arishaji, akaketi.

“Karibu mkuu, karibu sana,” yule fundi akamchangamkia kana kwamba wanajuana miaka mingi. Akaketi kwenye kibenchi huku akihakikisha jicho lake haliipotezi ile nyumba. Akavua viatu kumpatia, akimtaka kufanya haraka kidogo.

“Mtaa wa matajiri,” Amata akasema.

“Aaaaa ndo hivyo, matajiri wapate na masikini tufaidike!” yule fundi akamjibu.

“Hii nyumba ya nani?” akauliza.

“Ipi? Hiyo kubwa ya kizamani?”

“Yap! Napenda sana nyumba kama hizi, haiuzwi?” Amata akauliza.

“Haiuzwi hiyo kaka, kuna kijana mmoja anaishi hapo, zaidi hutembelewa na marafiki tu,” fundi akajibu.

“Watu wana raha zao bwana. Ni mfanya biashara au?” akazidi kuhoji.

“Dah! Hata sijui yaani, namuonaga kaingia, katoka bas…”

Mazungumzo kati ya Amata na fundi huyo yalichukua kama dakika thelathini hivi. Wakiwa wamezama kabisa katika mazungumzo hayo, Mazda jekundu likawasili katika lile geti na kupiga honi. Geti lilipofunguliwaa, gari lile lilijitoma ndani. Amata akaendelea kupiga soga na mwenyeji wake, wakiyasifia haya na kuyaponda yale kule. Kutoka ndani ya nyumba ile, hakuna aliyetoka muda huo wote ambao Amata amekuwa kwa fundi yule.

“Hapa naona sawa kaka!” yule fundi akamwambia Amata wakati akimsogezea vile viatu.

“Oh shukrani sana,” akamshukuru na kumpatia noti ya shilingi elfu mbili. Wakaagana, na Amata akaenda zake. Akiwa katika hatua fupifupi kulielekea gari lake, simu ikaita mfukoni. Akaichomoa. Akaitazama. Chiba.

“Yes!” akaitika.

“Kuna pandikizi…” Chiba akasema kutoka upande wa pili.

“Wapi?”

“Njoo, tukutane Makumbusho ya taifa,” Chiba akamaliza na kukata simu. Kamanda Amata, akasimama kwa sekunde kadhaa, akifikiri jambo. Ushirika kati ya ubongo wake na mwili ukachukua nafasi. Akajitoma garini na kuondoka haraka kuelekea huko kwenye miadi na TSA2.




Njoo, tukutane Makumbusho ya taifa,” Chiba akamaliza na kukata simu. Kamanda Amata, akasimama kwa sekunde kadhaa, akifikiri jambo. Ushirika kati ya ubongo wake na mwili ukachukua nafasi. Akajitoma garini na kuondoka haraka kuelekea huko kwenye miadi na TSA2.

* * *


Nyumba namba 73A


Mariamu aliketi kwenye kochi kubwa la vono. Bilauri iliyojaa mvinyo wa Dodoma ilikuwa mbele yake huku TV kubwa ikionesha kipindi cha Jiji letu Dar es salaam. Mbele yake, katika kochi jingine aliketi yule kijana aliyekwenda kumchukua kazini. Na dakika nyingine kama thelathini hivi akawasili mwanaume mwingine, pande la baba, akaungana nao. Hakuwa mwingine zaidi ya Brian Mkuchu.

“Poleni kwa matatizo…” akawaambia huku akiketi vyema kitini. Jicho lake lilikuwa likimwangali Mariam kwa tuo. Labda lilikuwa likiuburudisha moyo kwa uzuri wa mwanamke huyo.

“Tumeshapoa,” akajibu yule kijana.

“Mariamu!” Brian akaita. Yule mwanamke akageuka kwa pozi na kumtazama mwanaume huyo kwa jicho la ubembe.

“Labeka shemeji…”

“Naomba usiniite shemeji kuanzia sasa!”

Bila kutegemea kauli hiyo, Mariamu alijikuta akiangusha bilauri ile sakafuni na kuruhusu mvinyo yote kumwagika.

“…umekuwa adui yangu namba moja,” akamwambia.

“Shem, mbona sikuelewi?” Mariamu akauliza kwa kitetemeshi.

“Narudia, usiniite shem! Kwa nini umeificha siri tunayoitafuta muda wote? Mpaka jana mpumbavu anaingia ndani kwako kuichukua…”

“…Siri! Siri gani Brian?” Mariamu akatahayari.

“Ina maana Andy hajakwambia nini tunataka?” Brian akamuuliza kwa ukali.

“Hapana…” akajibu.

Briana akachomoa bahasha na kuchukua picha tatu akamuwekea mezani, “Nataka unambie huyo ni nani?” akamuuliza.

“Aka! Simjui mimi…”

“Umetusaliti, umetuingiza motoni, utatutambua. Utatueleza huyu ni nani…” Brian akamwambia kwa ukali. Akainuka na kuwasha luninga nyingine ndogo. Mariamu akashuhudia picha ambayo hakuitegemea. Yeye na Andy wakiwa kitandani kama walivyozaliwa, wakioneshana ufundi wote katika sanaa ya mapenzi. Baada ya dakika kama tano hivi picha ikawaonesha wamelala fofofo. Kwa sekunde chache Andy akaamka akionekana mchovu na kuchukua mkoba wake. Akachukua kitu kidogo sana na kukipachika puani kwa jinsi ambayo hakikuonekana kirahisi. Picha ile ikaonesha kila kitu kuhusu Amata na Chiba, walivyoingia mpaka chooni na kufanya kila walichofanya. Mpaka Amata alipoanza kupachua kamera za siri na alipompiga ngumi Andy ndipo ikazimika.

Mariamu akashusha pumzi. Akawatazama kwa zamu. Akavuta mkoba wake na kuinuka, tayari kwa kuondoka. Hakutaka hata kuaga mtu. Lakini azma yake haikufikia lengo, alijikuta kavutwa nyuma na kusukumiwa juu ya kochi. Kwa ukaidi wake akainuka tena, mara hii, Brian akamnyanyua kama karatasi na kumtupa juu ya meza. Mariamu akapiga yowe la maumivu huku meza ile ikipasuka vipande. Kwa kitendo kile, Andy hakuweza kuvumilia. Akainuka na kutaka kumshika Brian, hakuweza. Konde moja la kilo nyingi likamrudisha chini.

“Lazima mjue kuwa nimekuja kwa kazi maalumu, na ninyi wawili mmeniharibia. Andy, kwa nini ulishindwa kuwapiga risasi wale jamaa na hukuwa umelala? Ulidanganywa na huyu Malaya? Tutakufanya kama tulivyomfanya Dastan,” Briana akaunguruma. Mkanda mkononi. Akamtazama Mariamu.

“Unambie wale ni akina nani?” akamuuliza na kuanza kumtandika kwa mkanda ule bila huruma. Hasira iliwaka ndani ya Brian hakukuwa na wakuizuia. Mariam hakuweza kujitetea zaidi ya kulia mpaka sauti kukauka. Mwanaume yule hakujali, aliendelea kumsulubu kwa mikanda mpaka aliporidhika.

“Utamuua Brian, mtu ukishampiga hivyo na hajakwambia kitu ujue ni innocent!” Andy akasema.

“Unanifundisha kazi? Wewe Andy ni mzembe. Ulishindwaje kulichukua lile faili pale ofisini kwako mpaka kile kibibi kinakuzidi maarifa? Sehemu ya pili ya ile siri, je; sote tulijua kuwa imefichwa na Dastan…” akahema kwa nguvu “tukafanya yote kujua anayeishi pale ni nani, tukampata, ukamlaghai kwa mapenzi ukampata, badala ya kufanya kazi mapenzi yakakulevya. Faili linguine linaibwa hapo hapo unaona kwa macho…. You are so stupid. Ninyi wawili mmepanga, sasa mtakiona,” Briana akabwata mpaka Andy akaogopa. “Toa huu mzoga wako, kaufunie stoo, usiku huu tutauzika mimi na wewe!” akamwambia huku tayari mkononi keishakamata bastola. Andy hakuwa na jinsi akamtazama Mariamu akiwa pale chini, nguo yake yote ikiwa imetota kwa damu. Kimya. Dalili ya uhai haikuwapo. Hakuweza kumwinua, akamburuza mpaka stoo. Akiwa katika kumweka sawa, akajikuta akipigwa na kitu kizito. Andy akayumba na kujibamiza ukutani, akaanguka juu ya Mariamu. Brian akaondoka na kutokomea kusikojulikana.

?



Makumbusho ya Taifa


Kamanda Amata aliegesha gari nje ya lango kuu la jengo hilo. Akateremka na kuufunga mlango nyuma yake. Sekunde tano zikamtosha kutazama huku na kule kama kuna lolote baya kwa upande wake. Hamna. Akavuta hatua na kuingia katika uwanja wa jengo hilo. Hakukuwa na watu wengi kwani tayari muda wa kufungua ulikuwa umekaribia sana. Ni Wazungu wachache tu waliokuwa wakirandaranda na kupiga picha hii na ile. Akazikwea ngazi na kujitoma ndani.

Ndani ya jengo hilo kulikuwa na mambo mengi ya kihistoria hususan juu ya taifa la Tanzania na Tanganyika ya zamani. Historia za watawala na watawaliwa katika uga tofauti. Chiba alikuwa amesimama mbele ya picha kubwa iliyosheheni maandsihi mesngi ya Kiingereza na Kiswahili. Amata akasimama karibu yake.

“Kuna lolote?” akamuuliza.

Chiba badala ya kujibu, akaondoka eneo lile. Amata naye akamfuata. Mguu kwa mguu mpaka

katika chumba kingine, wakaingia ndani. Chumba hicho kilikuwa ni ofisi yenye kila kitu kinachostahili kuwapo ofisini. Palikuwa na viti viwili tu; yaani cha mwenye ofisi na cha mgeni wake. Chiba moja kwa moja akaenda kuketi kwenye kile cha mwenye ofisi na Amata akaketi kwenye kile kingine.

Upande ule, Chiba akavuta droo na kutoa picha nne, akamwekea Amata mezani.

“Unamkumbuka?” Chiba akamuuliza. Amata akatazama ile picha kwa makini sana.

“Si ni yule bwege wa leo!”

“Good! Anaitwa Andrew Makita,” Chiba akamwambia.

“Andrew Makita!” Amata akalirudia jina lile kwa mshangao na kumtazama Chiba.

“Mbona unashtuka? Unamjua?”

“Simjui kwa sura ila kwa jina namjua kuwa ni mwanakondoo…”

“Anafanya biashara…” Chiba akasema. Amata akabaki kimya, akamkazia macho TSA2.

“Unataka kuniambia, huyu dogo ana linki na hawa majahili…”

“Swadakta!” Chiba akaitikia, “Kwa tafutishi nyingine nilizozipata katika ile bahasha… huu mtandao ni hatari,. Bado wana azma ya kuipindua serikali iwe kwa maji au kwa damu. Wamepanga kuwa, kama wameshindwa kwa kutumia bunduki basi watakuja kwa njia nyingine. Mapinduzi yao ni awamu tatu. Awamu ya kwanza walishindwa mwaka 1964, awamu ya pili wakashindwa tena mwaka 1980. Sasa awamu ya tatu wamepanga kuja kivingine. Maadam serikali imeamua kuruhusu mfumo wa vyama vingi, basi wamejificha kupitia humo. Plan A ilikuwa ni kuiangusha serikali kwa kutumia sanduku la kura, inaonekana hii ni ngumu. Plan B ni mbaya Zaidi…”

Amata akabaki kimya kusikiliza kwa umakini wa hali ya juu. Lakini aliposikia kuwa plan B ni mbaya hakuweza kutulia kwani kama kuna kitu kilikuwa hakipendi basi ni wananchi wasiyo na hatia kuingia matamatanui kwa tamaa za watu wachache.

“Ubaya upi?” akauliza.

“Hili genge limejiwekea nadhiri kuwa, endapo litashindwa kwenye sanduku la kura mara tano mfululizo, litaingia msituni…” Chiba akasema na kuweka tuo. Amata akamkazia macho kwa yale anayoyasikia.

“Nchi hii hii au nyingine?” akauliza.

“Hii hii,”

“Aya, ngoja tuone. Enhe… na nani anyewafadhili?” akaongeza swali.

“Amata, hii taarifa haijakamilika. Inaonekana Dastan hakufanikiwa kuipata yote, hivyo hatuna budi kutembelea nyumba namba 73A… kwa sababu kaizungumzia sana katika taarifa hii,”

“Mtaa wa Galu,”

“Yes!”

“Leo leo usiku…”

“Naunga mkono,” Chiba akajibu. Akarudishia droo na kuifunga kwa ufunguo kama mwanzo. Ukimya ukajidai kati yao kwa jozi la sekunde.

“Hayo ni yote kwa leo…” Chiba akamwambia Amata huku mikono yake yote miwili ikiwa juu ya ile meza.

“Andrew Makita, inabidi akacukuliwe apelekwe shamba haraka iwezekanavyo. Hawezi kuidoublecross serikali yake…” Amata akasema, “Leo tuna kazi mbili kubwa, kumtia mkononi Andrew na lazima lifanyike jioni hii. Pili kufanya black bag Mtaa wa alu namba 73A,” akamalizia.

“Haswaa, nilikuwa nasubiri mpango kazi, maana nakujua, ukishasikia haya huwezi sema kesho wala kesho kutwa,” Chiba akamwambia Amata.

“No! Chiba,” Amata akawa kama mtu aliyegutushwa.

“Ndiyo kaka…”

“Twende Galu sasa hivi…” akamwambia.

“Kamanda, kweupe sana,” akaitazama saa yake, ikamwambia ni saa tisa na dakika thelathini alasiri,” Chiba akatia shaka kwa hilo.

“Nina maana yangu kusema hivyo Chiba! Leo mchana nilimuungia mkia huyu bwana, kutokea Ilala DSJ maana mpenzi wake ni staff pale. Na safari yao iliishia kwenye hiyo nyumba. Nafikiri ni vyema twende sasa, la kutokea litokee, twende,” Amata akamwambia Chiba.

“Sawa, ila hapa nimetembea kizembe Kamanda…” Chiba akasema akimaanisha hana silaha.

“Hata mimi, twende ofisi ndogo tukafunge mzigo,” Amata akamwambia.

Wote wawili wakainuka na kutoka nje ya jengo hilo. Wakaingia garini. Moja kwa moja mpaka ofisi ndogo. Madam S alikuwa bado ofisini akiendelea na majukumu ya serikali. Alipowaona vijana hao akapata tashwishwi ya kutaka kujua kulikoni. Kwa maana katika ofisi hii, huja kwa kuitwa au hutoa taarifa.

“Nyie vipi? Mmefumaniwa?” akawauliza.

“Hapana, tunaenda vitani…” akamjibu huku akivuta mlago wa kabati baada ya kuufungua ule wa chuma. Madam S akainuka na kutoka pale mezani, akawafuata.

“Nyi’’ watoto mbona siwaelewi?”

“Tupo kazini mama, tunaenda Mtaa wa Galu, nyumba namba 73A. lolote linaweza tokea, usilale…” Amata akamwambia Madam S huku akimpa Chiba shot gun iliyoshiba risasi na bastola moja. Na yeye akachukua kama hivyo hivyo. Akafunga lile kabati na kumgeukia bosi wake.

“Kuna mjukuu wako anafanya ujinga, tunaenda kukuletea popote alipo…” akamwambia na kumpigia saluti. Madam S alishazoea utani wa TSA 1 hata wawapo kazini. Lakini alimjua vyema awapo sirias na awapo katika utani. Siku hii alimsoma kijana wake na moja kwa moja akajua kuwa kuna jambo zito.

“All te best!” akawaambia. Amata na Chiba wakapotelea nje. Mwanamama huyo akaifuata lunina yake na kuiwasha kamera inayoonesha matukio ya nje kwenye maegesho ya magari. Akawaona vijana wake wakiingia garini haraka haraka na kuondoka.

“Mh!” akaguna na kujishika kidevu kwa sekunde kadhaa, akifikiria jambo. Kilichomtatiza mwanamama huyu ni jisi vijana hao walivyoingia na kuondoka. Ijapokuwa mapambano yote ya silaha hupangwa mezani lakini yapo yanayotokea kwa nasibu tu na haya humtaka mtu kujihami mwenyewe. Hili hakulielewa kabisa. Akavuta hatua na kuiendea simu yake ya mezani. Akaminyaminya tarakimu Fulani na kuiweka sikioni.

“Hello, Gina!” akaita na kuitikiwa upande wa pili.

“…”

“Fika Mtaa wa Galu, nyumba namba 73A, kachunge mikia ya kaka zako kule…” akakata simu na kuirudisha katika kitako chake. Akaiendea meza yake na kuketi kitini.

* * *

Brian alitulia kimya katika ndani ya baa ya Mwanamboka eneo la Kinondoni. Akili yake ilikuwa imetibuka, aliwaza hili akawaza lile. Hakupata jibu. Aliona wazi kuwa Andrew kamfanyia hujuma. Lakini bado akawaza kuhusu Mariamu. Mariamu alijua kuwa pale ndani pana siri akaiuza kwa watu wengine. Hapana.mawazo yaligongana, fikra zikashindwa kuwa kitu kimoja. Brian akagutuliwa na simu yake ya kiganjani iliyoita kwa fujo. Alipotazama kwenye kioo, akasoma, ‘Babu’. Moja kwa moja akajua kuwa mwito huo una maana yake. Akainuka haraka na kuiacha ile pombe yake mezani. Haikuwa na maana tena.

Ndani ya gari lake, Mazda, jekundu, Brian akatulia tuli. Akafyatua simu yakena kuiweka sikioni.

“73A”akaitikia.

“Code 005, Amata Ric, Unstopable human being. Brian, htumepata kumtambua mtu mwenye uficho wa code hiyo ya 005. Yupo hapo hapo Tanzania, ni mtu hatari sana. Tumetazama rekodi zake kwenye kabrasha za mashirika ya kijasusi duniani, MI6 wamemueleza kama mwaDanamu hatari mwenye kasi ya ajabu katika mapambano. Interpol nao wanamfahamu kama ‘Thorn’ yaani mwiba ambao ukikuchoma kupona ni kitendawili…” mtu wa upande wa pili akaeleza kwa sauti ya taratibu.

Brian akajikuta akipatwa na ubaridi mkali kuanzia unyayoni mpaka utosini. Akashusha pumzi ndefu. “Kwa hiyo unaniambiaje? Maana kuna ripoti nilikuwa naiandaa nikuletee ya huyu mpumbavu Makita,” Brian akaeleza.

“Kwanza kabisa, ili tufikie lengo letu mwaka huu, huyu 005 lazima auawe hata kama ni kwa kumroga,” sauti ile ikamwambia ikiwa kwenye mwangwi ili isitambulike kiurahasi. Brian akapumua kwa nguvu. Kisha akamweleza kila kitu kilichotukia siku hiyo.

“Kwa hiyo, Andrew Makita anataka kufanya kama Dastan? Sawa maadam umesema yupo ndani, nenda ukamuue sasa hivi kisha myeyushe kwa tindikali asionekane tena duniani…”

“Ok Sir!” Brian akajibu.

“Shughulika na huyo Andrew, muache huyo mwanamke ili umtumie kama chambo cha kumpata huyo mpumbavu mwingine,”ile sautio ikamwambia.

“Copy!” akakata simu na kulisha gari lake. Akatoka kwenye maegesho na kuingia barabara kubwa ya Kawawa kuelekea Morocco.

* * *




Shughulika na huyo Andrew, muache huyo mwanamke ili umtumie kama chambo cha kumpata huyo mpumbavu mwingine,”ile sautio ikamwambia.

“Copy!” akakata simu na kulisha gari lake. Akatoka kwenye maegesho na kuingia barabara kubwa ya Kawawa kuelekea Morocco.

* * *

Kamanda Amata na Chiba wakawasili katika ile nyumba. Wakateremka na kuliacha gari umbali mdogo kutoka katika geti la nyumba hiyo.

“Kazi moja tu!” Amata akasema.

Chiba akaitikia kwa kichwa, wakavuta hatua kulielekea geti la nyumba hiyo. Hakuna aliyeongea. Silaha zao zolikuwa zimefichwa kwenye makoti waliyovaa, usingeziona. Walipoukaribia mlango, ghafla kwenye kona, likaibuka Mazda jekundu. Amata akampa ishara Chiba, wakajifanya wapita njia, wasisimame kwenye lile geti. Lile mazda likafika getini. Geti likafunguliwa kwa mtambo maalumu na kisha kujifunga mara tu baada ya gari lile kuishilia ndani. Amata na Chiba wakatazamana. Wakaizunguka ile nyumba na kugundua kuwa ilikuwa imepaka na nyumba nyingine ambayo haikuonekana kuishi watu. Upande huo haukua na mambo mengi. Amata akaitazama ile nyumba pweke, nyasi na magugu viliotea ndani yake. Akauendea mlango na kujaribu kuusukuma, ukafunguka, wakaingia ndani na kupambana na nyasi ndefu, magugu na nyuzi ngumu za buibui. Ukuta wa nyumba hii ulipakana na ule wanaoutaka. Katika yake kulikuwa na uchochoro wa mita moja hivi.

“Hapa panatufaa!” akamwambia Chiba. Wakajiweka tayari kukwea ukuta ule. Haukuwa mrefu sana, kama mita tatu na nusu hivi. Kamanda Amata akajiweka sawa, akakinga mikono yake kwa nyuma. Haraka Chiba akaelewa nini cha kufanya. Akaweka mguu wake katika viganja vya Amata, akajiinua na kuuweka mwingine kwenye bega. Akakamata ukuta ule sawia na kujivuta haraka juu huku akiuacha mguu wake ukining’inia. Amata akaukamata ule mguu na kuutumia kukwea ukuyta ule mpaka juu. Walipokuwa juu, wote kwa pamoja wakajirusha mpaka ukuta wa pia na kutua ndani ya wigo huo kwa ustadi mkubwa na kutulia kimya. Tukio hilo lilichukua sekunde kumi tu. Walipoona kuna ukimya na utulivu wa kutosha wakainuka na kila mmoja akapita upande wake, wakakutana mlango mkubwa.

Ndani ya nyumba hiyo, Brian alisikia mchakacho wa viatu. Nina wageni! Akawaza na kuiendea droo kubwa ya mezani, akatoa bastola na kuiweka sawa, tayari kwa lolote. Akajibanza nyuma ya kabati lilikuwa jirani kabisa na mlango mkubwa.

Nje ya nyumba hiyo, Chiba alikuwa wa kwanza kuufikia mlango. Amata akabaki nyuma na kuiweka tayari ile shot gun yake. Chiba akatoa ishara kuwa anaingia, Amata akatikisa kichwa kumwonesha kuwa yuko sawa kwa kumlinda. Mchezo wa hatari. Akaruka kwa guu lake la kulia na kuvunja mlango ule. Ukaachana vipande viwili, akachomoa bunduki yake na kuiweka sawa. Ndani kulikuwa kimya.

Tunapambana na mjuzi! Chiba akawaza na kuanza kuvuta hatua kuingia ndani. Brian alijibana palepale pasina kutikisika. Alianza kuona kivuli cha mgeni wake kikitangulia kabla ya mwenyewe kuingia ndani. Sekunde chache baadae, akamwona mtu huyo akizama ndani na bunduki yake ikiwa mbele kabisa. Kwa macho ya harakaharaka, Brian aliona jinsi bunduki ile ilivyoshikwa kikakamavu. Taratibu akaamua kuiweka bastola yake kibindoni ili amfanyie shambulizi la kushtukiza. Ikawa hivyo. Brian aliruka na kutua kwenye shingo ya Chiba kwa pigo moja la karate. Chiba hakupata nafasi ya kujitetea kwa pigo hilo. Alipogeuka alikutana na pigo lingine lililotua kwenye chembe ya moyo. Akapepesuka na kuanguka vibaya sakafuni. Brian alikuwa akijipanga kuiendea ile bunduki ya Chiba, hakuwahi. Ghafla alijikuta mikononi mwa Kamanda Amata. Mapigo saba yenye kasi ya ajabu yalimwacha hoi sakafuni akiwa hajiwezi. Brian akiwa chini sakafuni alihisi kama kapigwa kwa chuma. Akakusanya nguvu zake zote na kuinuka kumkabili Amata. Amata akasimama kimya akimtazama jinsi anavyojipanga. Akarusha mapigo mfululizo kumwelekea Amata lakini yote yakaepwa kwa ustadi kabisa. Kamanda Alikuwa akitafuta nafasi tu na alipoipata akapeleka pigo la nguvu kwenye chembe ya moyo. Brian alipotaka kukinga, akachelewa. Pigo lingine la karate likatua kwenye koromeo. Amata akaruka kimo cha ng’ombe na kumtandika teke la mbavu lililompeleka chini. Brian alitambaa mita kama tatu akageuka ghafla na bastola mkononi. Amata akaruka kandona sisasi tatu zikapita nukta chache kutoka pale alipoangukia. Sekunde hiyo hiyo akashuhudia kichwa cha Brian kikifumuka vibaya na mwili wake kusukumwa kando. Amata alipogeuka nyuma, macho yake yakamtazama mwanamke mrembo aliyesimama katikati ya mlango huo. Gina.

“Muwe mnaaga mnapoondoka,” Gina akasema huku akiipachika bastola kiunoni mwake.

“Tungekuwa hatujaaga ungejuaje kama tuko huku?” Amata akamjibu huku akinyanyuka na kumwendea Chiba aliyekua akiinuka taratibu huku bado anakohoa.

“Vipi kaka uko poa?” Amata akamuuliza.

“Yea, mpumbavu aliniotea huyu…” akasema wakati akisaidiwa kuinuka. Amata na Gina wakaanza msako wa chumba kimoja baada ya kingine. Kila kimoja kilikuwa tupu, sanasana ni picha na vijatabu mbalimbali. Kila walipokuwa kitabu cha kumbukumbu walikibeba. Amata alipoutikisa mlango wa stoo akakuta mgumu haufunguki. Akaupiga teke, ukafunguka na kujibamiza upande wa pili. Aliyoyaona hapo, mwili ulimsisimka. Miili ya watu wawili, anaowatambua, aliowafuatili mchana wa siku hiyo. Andrew Makita na Mariamu walikuwa wamelaliana. Wamekufa? Akajiuliza. Akavua saa yake na kuuchukua mkono wa kushoto wa Andrew. Akafanya kama anamvesha. Akabana vyema na kuwasha nobu ya kusoma mapigo ya moyo. Ikamwonesha kuwa kijana huyo bado mzima ila yupo katika mzimio mzito. Akafanya hivyo na kwa yule mwaDanada pia, vivyo hivyo. Haraka akamtaka Gina kuleta gari. Dakika mbili tayari gari ilikuwa pale ndani ya wigo. Wakasaidiana kuwapakia wote wawili.

“Mpigie simu Jasmini, tukutane shamba,” Amata akatoa maagizo. Gina akaingia garini na kuondoka kwa kasi kuelekea shamba na kuwaacha vijana wale wakiwa bado katika ile nyumba. Chiba aliendelea kupekua hapa na pale, akachukua hard disc ya kompyuta na makabrasha mengine muhimu. Akabomoa sefu moja iliyowekwa kwa siri nyuma ya ukuta na kufunikwa na picha kubwa ya kisiwa cha kuvutia. Wakachukua kila kilichomo ndani.

“Safi, unajisikiaje sasa?” Amata akamuuliza Chiba.

“Bado sipo vizuri sana…”

“Ok, Jasmin atakufanyia uchunguzi. Tuondoke zetu!” Amata akamwambia Chiba. Kabla ya kutoka Chiba akatega kamera yake ya siri ambayo aangeweza kuifuatilia kutoka umbali wa mita mia tano na pale ilipo. Wakatokea getini na kulifunga vizuri. Wakaingia garini na kuondoka zao. Amata akapiga simu kwa Madam S.

“Mission clear! Mwambie Simbeye aende kuna mzigo wake. Hiyo nyumba iwe chini ya ulinzi wa siri mpaka tutakaposema,” Amata akamwambia bosi wake.

“Sawa, linafanyiwa kazi… uelekeo wapi? Nataka kupata taarifa ya uvamizi wenu,” Madam S akamwambia Amata.

“HOT, tunaelekea shamba, tuko na wafu wawili tunataka kujaribu kuwafufua ili watugee waliyonayo. Hapa tuna tafutishi za kutosha ambazo nafikiri zitatupa njia sahihi ya kulibomoa hili genge,”

“Safi sana TSA1, tutakutana huko saa mbili zijazo,” Madam S akajibu na kukata simu.

* * *


SAA 6 BAADAE


Akili, moyo na mwazo ya Mc Tee havikutulia kabisa. Katika Utaratibu wa kazi walivyojiwekea ni kwamba, ikipita saa sita simu yako haipokelewi basi maana yake umeshakufa au haupo salama. Kwa mara ya kwanza, hakutaka kukubaliana na hilo ijapokuwa ndiyo Utaratibu wao wa kazi. Akaitazama saa yake, muda unayoyoma. Nini kimetokea hajui. Simu ya mwisho kwa Brian ilikuwa ni kumpa maelekezo ya mtu wa kummaliza, code 005. Na sasa Hakuna jibu. Amekufa? Akajiuliza. No labda amekamatwa! Akajifariji. Akatembeatembea barazani huku akiangalia maji ya bahari yanavyoyumbayumba kwa madaha. Wala hali ile haikumpa ahuweni ya mawazo. Yalisongeka haswa.

Akaamua kurudi ndani na kuketi kwenye ofisi yake ndogo, ambayo kwayo walikutana na watu wake si chani ya saa hamsini zilizopita. Akawasha kompyuta na kuwaita wote. Walipokuwa online mazungumzo yakaanza.

“Bandari salama si salama tena,” akawaambia.

“Kwa vipi comrade?” Big J alikuwa wa kwanza kuuliza kwa shauku.

“Brian hayupo hewani kwa saa saba sasa,” akawaambia.

Wote wakaelewa mara moja nini anamaanisha. Wakasikitika kwa sekunde chache kisha mazungumzo yakaendelea.

“Jesca, nafikiri huna budi kwenda Dar… na kwa kuwa tayari ulikuwa na hilo moyoni, ruksa,” Mc Tee akamwambia.

“Sawa comrade nitafanya hivyo,” Jesca akajibu.

“Yatupasa kuwa makini, maana top ranking tunakwisha. Kama wameweza kunasa zile siri pale ndani mjue kuwa kazi tunayo,” Mc Tee akawaeleza.

“Mkakati upoje?” Big J akauliza.

“Tuwe kimya kabisa, tusubiri Jesca atatuambia nini. Mimi nitaondoka kesho kuelekea Urusi kukutana na mkulu kisha nitawaunganisha kwa tamko la mwisho,” Mc Tee akawaambia wenzi wake kisha simu ikakatwa na kila mmoja akatakiwa kufanya kadiri ya maagizo hayo ya awali.

Mara baada ya simu ile kukatwa, Mc Tee alijitupa kochini na kujinyoosha. Akavuta simu yake na kupekua namba zilizopo. Baadae akafanikiwa kuipata ile aitakayo, kampuni ya ndege. Kwa kuwa pesa haikuwa tatizo kwake, aliweza kupata tiketi ya siku inayofuata katika kampuni ya KLM. Baada ya kuhakikisha kuwa amekamilisha malipo yote, akaandika memo ndogo na kuipeperusha mpaka kwa mwenyeji wake kuwa yupo njiani.




ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

BLOG