Search This Blog

Saturday, February 26, 2022

SIHITAJI KURUDI NILIKOTOKA - 3

   

Simulizi : Sihitaji Kurudi Nilikotoka 

Sehemu Ya Tatu (3)


" tuliahidianaje kuhusu weekend ya leo?.

" kwenda club night.

" So!. Alidakia tunu.

" Um jaman!, kwani hakuna jambo unaloweza kupanga kufanya kisha ukalighairisha?.

" Kwa iyo ushaghairisha.

" Ndio.

" kwa sababu ya huyu mshamba mshamba.

" Nisikilizeni nyie viumbe, kila mtu ana maisha yake humu ndani, msimwite mtu mshamba hali ya kuwa hamjui anasumbuliwa na nini!, nna iman lucky si mshamba wala sii wa kuja kama tunavyomdhania, kama nyie hamko tayari kubadilisha nia yenu ya kumnyanyapaa, mimi ntakula nae sahani moja na naitaji kumsaidia kuhakikisha anarudi katika hali yake ya kawaida. Ntatoka nae leo kwa kuwa amenikubalia, nyie tokeni tu mi siko pamoja nanyi leo. Alisema maryam.

" Leo hiyo we ni wa kuzungumza hivyo. Aliuliza amina.

" yah, lucky ni rafiki yangu, na ntafanya juu chini, hata pesa ntatumia ili siku moja nijue kitu gani kinamfanya akose raha.

" Sawa jitahidi. Alisema tunu.

" Mkishuka chini mtasikia story zake alichokifanya ndo mtajua kama ni mshamba au sii mshamba. Alisema maryam.

Lucky alitoka bafuni akiwa ametakata usoni, hawakuendelea kuongea wakakaa kimya, lucky alijipangusa akajiweka vizuri mwili wake akavaa nguo za kawaida alizozoea, maryam nae alivaa wakajiweka sawa kwa ajili ya kuondoka, kabla ya kutoka lucky aliwauliza wakina amina kama hawana safari yoyote kwa weekend hiyo ili ikiwezekana watoke wote, ila walikuwa wazito kumjibu maryam akamuitaji aachane nao wasepe zao..


Walipokuwa wanashuka ngazi kuelekea chini, maryam alitoa paswed cm yake ya iphon akaandika ujumbe mfupi ulioonekana kwenda kwa Sophia msimamizi wa wanafunzi wa chuo kiranja.

** Sophy, natoka na Lucky, nimefanya hivi ili kumbadilisha mazingira niangalie itakuwaje, naomba tushirikiane kumshawishi awe na furaha sii unaona yeye pekee ndo mwenye hali ya unyonge chuoni hapa?.


Kabla ya kuituma kuna cm iliingia, alifurahi baada ya kuona jina la mdogo wake wa mwisho, alipokea akaweka sikioni.

" Hellow my lovely sista.

" hellow too Shikamoo sista.. Sauti ya upande wa pili.

" Marhabaa how are you.

" Im cool and you.

" im okey umenikumbuka?.

" yah dada nimekukumbuka.

" uko nyumbani?.

" ndio nimekaa na mama.

" wow!, nakuja muda si mrefu nimewamiss sana, mwambie mum aongee na witty waandae chakula kizuri nakuja na rafiki yangu.

" Ok sista ntamwambia.


Cm ilikatika akaisend message kuelekea kwa sophia.

" Nyumbani ni wapi?. Aliuliza lucky.

" Ni mbezi beach samaki.

" kumbe mbali hivyo.

" No bhna. Tunachukua tax fasta tu hapo.

" unachezea pesa hivyo, kwa nini tusipande dala dala tukatumia elfu moja badala ya elfu 20.

" jasho la watu huwa sipendi.


Alisema maryam lucky akawa amefikiria kitu moyoni mwake na kuachia tabasam, walitoka hadi kwenye kituo cha tax wakachukua tax na kuanza safari, lucky mkononi alishikilia cm kubwa ya sony, maryam alikuwa na iphon ambayo aliitach kila wakati kutokana na message zinazoingia, alikuwa anapenda sana kuchart kuliko maelezo, moja ya watu aliokuwa anachart nao ni sophy ambao walikuwa wanachart kuhusu lucky kuweza kumrudisha katika hali yake ya kawaida, baada ya kugundua uenda kuna kitu kwenye maisha yake kimemuharibu kisaikologia kwa jinsi walivyomuangalia kwa haraka haraka hasa kwa tukio zito aliloweza kulifanya...


Walifanikiwa kufika mbez beach samaki kwenye mishale ya saa saba na nusu, familia nzima ya maryam ilikuwa nyumbani isipokuwa baba yake, waliingia ndani wakapokelewa kwa furaha za hali ya juu, Chakula kilikuwa tayari ikabidi kabla hata ya kupumzika wapate msosi, walipomaliza wote walikusanyika sebleni kupiga story, Maryam alitumia muda huo kumtambulisha lucky kwa mama yake pamoja na wadogo zake wawili waliokuwepo.

" Mama huyu anaitwa Lucky, ni mwanafunzi mwenzangu chuoni, tunakaa chumba kimoja, chake ni changu changu ni chake. and lucky huyu ndo mam wangu, hawa ni wadogo zangu na huyu Witty ni dada yangu yuko hapa kwa ajili ya kusaidia kazi si unajua.

" Yah!, nimefurahi kuwafahamu wote.

" Mimi pia nimefurahi sana kukufahamu binti.

" Asante. Alisema Lucky.

" Hatujaja hapa kukaa sana, nimekuja kuwaona tu na kuondoka sababu kuna sehemu tunaenda, Sauda.. Alisema maryam kisha akamuita sauda mdogo wake wa mwisho.

" Abee.

" Nenda kwenye meza ya chakula ukachukue mfuko nlokuja nao kuna zawadi yako na ya Farhat mule ndani.

" Sawa ila vibaya hivyo dada ina maana mnaondoka muda huu?.

" Yah.

" Nimekumiss dadaangu nataka kukaa na wewe.

" Usijali weekend ijayo ntakuja kushinda nyumbani.

" kweli?.

" Bhna kachukue huo mfuko usinitie wazimu. Sauda aliinuka akaenda kuchukua mfuko alioambiwa kwenye meza ya chakula.

" Baba na leo kaenda kazini?. Aliuliza maryam.

" Hapana kuna sehemu tu kenda. Si unajua baba yako asivyoisha mihangaiko.

" Mh! Aya sawa.

" Binti mbona umekaa kimya sana. Mama maryam alimuuliza lucky.

" Hapana kawaida tu mama usijali.

" Alafu mbona kama nliwahi kukuona sehemu au nimekufananisha?

" mimi?

" Yah.

" Labda. Siwezi kukataa wakati sijui wapi.

" Wee ni mtoto wa mzee Edwad yule mwenye kampuni ya magari kariakoo kwa wahindi au sie?. Aliuliza mama maryam swali lililomfanya lucky ajiulize maswali mia kidogo yasiyokuwa na majibu, mzee huyo kweli ndo alikuwa baba yake mzazi, ilibidi ajiulize amemjuaje na aliwahi kumuona wapi.

" mzee edwad hapana. Aliamua kukataa kutokana na kusikojua wala kukumbuka alimuona wapi, isije kuwa alimuona sehemu za uchafu uchafu katika enzi zake then akakubali tu heshima ikapungua.

" Ok samahani basi nlikuwa nimekufananisha. Maana yule mzee ana mtoto wake umefanana nae sana.

" Okey, itakuwa tumefanana tu duniani wawili wawili.

Maryam alikuwa anamuangalia mama yake kisha lucky jinsi anavyopokea maneno, kwa akili ya haraka haraka kuna kitu alikigundua machoni mwa lucky pindi alipoulizwa kuhusu mzee edwad, alihisi uenda ni kweli kwa jinsi lucky alivyolipokea jina la mzee huyo, ila hakutaka kuyaendeleza akaliweka moyoni ili siku nyingine aje ambane mama yake kuhusu huyo mzee..


Walitaniana na kucheka kama familia ndani ya lisaa limoja na nusu, furaha yao ilimtesa sana lucky aliekuwa anakumbuka maisha flan ya nyuma hasa baada ya kutajiwa jina mzee edwad, aliikumbuka familia yake ambayo hajaiona mwaka na zaid, hakujua lini ataiona, maryam aliingia chumbani kwake akachukua funguo za gari na kumuomba lucky waondoke, waliaga wakatoka nje na kuingia ndani ya gari.


Maryam alipoliwasha lucky alimuangalia kumbu kumbu za mawazo yake zikaenda mbali kidogo, akakumbuka baadhi ya vitu alivyokuwa anafanya kabla ya kuwa Lucky kama lucky, maryam hali ya lucky kuwa na mawazo aliiona, alimuita na kumuita tena lakini hakuitika, walipofika nje ya geti alimgusa begani akashtuka.

" Nini lucky?. Nini unawaza namna hiyo nakuita mara kumi kumi huitiki.?

" I'm Sorry maryam, nlikuwa mbali sana kimawazo.

" kitu gani ulikuwa unawaza.

" Soon utajua.

" Unanipa wakati mgumu ujue na sipendi unavyokuwa hivyo dia serious, Nkuombe kitu?.

" Yah.

" Naomba tupite kwenu tukasalimie pliz!. Alisema maryam kumtest lucky kisha akasikilizia atajibiwa nini.

" Siku nyingine usijali.

" Kwa nini isiwe leo?.

" Huwa napenda nkiongea na mtu mara anielewe.

" Ok poa.


Hakuitaji kwendelea na mada hiyo, aliamini mtu mwenyewe anaeongea nae kichwa chake nusu zimo nusu hazimo, walienda hadi msasani wakapita moja ya duka kubwa la nguo kufanya shoping ndogo, walipomaliza walienda moja kwa moja beach kuangalia mazingira na kuogelea pia.

" Napenda sana kuogelea sijui na wewe vipi?. Alisema maryam wakiwa ufukweni mwa bahari.

" Sii saana. Napenda tu kuyaona maji na kuyachezea chezea basi.

" poa, mi nakuacha hapa basi naingia kwenye maji japo dakika tano nikatoe mikosi.

" Usijali kuhusu hilo best.

Alivua nguo zake akabaki na nguo za ndani, alitoa kimtandio kwenye mkoba akajifunga kiunoni chengine kichwani, lucky alimwangalia bibie alivyo na mwili mzuri wa kuvutia, alimsifia maryam akaelekea zake kwenye maji, alipofika alijitupa akazamia ndani na kwenda hadi kwenye maji makubwa.




Hakuitaji kwendelea na mada hiyo, aliamini mtu mwenyewe anaeongea nae kichwa chake nusu zimo nusu hazimo, walienda hadi msasani wakapita moja ya duka kubwa la nguo kufanya shoping ndogo, walipomaliza walienda moja kwa moja beach kuangalia mazingira na kuogelea pia.

" Napenda sana kuogelea sijui na wewe vipi?. Alisema maryam wakiwa ufukweni mwa bahari.

" Sii saana. Napenda tu kuyaona maji na kuyachezea chezea basi.

" poa, mi nakuacha hapa basi naingia kwenye maji japo dakika tano nikatoe mikosi.

" Usijali kuhusu hilo best.

Alivua nguo zake akabaki na nguo za ndani, alitoa kimtandio kwenye mkoba akajifunga kiunoni chengine kichwani, lucky alimwangalia bibie alivyo na mwili mzuri wa kuvutia, alimsifia maryam akaelekea zake kwenye maji, alipofika alijitupa akazamia ndani na kwenda hadi kwenye maji makubwa.


Songa nayo......


Alikuwa anayajulia vizuri kuyachezea ya mbali na karibu, eneo alilokuwa analitumia kuogelea kulikuwa na kikundi cha vijana nao wakifanya yao, walipomuona mtoto mzuri anaoga waliitaji kumfata ili wakaoge nae, walimsogelea wakampa Hi, maryam hakupenda kitendo hicho akawaomba wakae mbali nae haitaji, walimng'ang'aniza wakawa wanamshika shika hasa kwa kuwa walimuona yeye peke yake hana mtu.

" Naomba mniache basi nyie vipi.

" Aaaah mtoto mzuri hutaki nini sasa?.

" Tueshimianeni kila mmoja anakuja huku kwa starehe zake tafadhali.

" Oya mnamuelewa huyu?.

Walimzunguka wakawa wanamtupia maji usoni huku wakiwa wanacheka kwa furaha, wengine walizamia chini na kumshika mapaja yake, maryam alilalamika haitaji kitendo hicho akawaonesha uso wa kuchukia lakini wapi, alipoona wamezidi ilibidi aanze kuwamiminia matusi ya nguoni bila kuogopa, vijana hao ambao walikuwa watano hawakufurahishwa na kitendo cha maryam kuwatukania wazazi wao na matusi mengine makubwa huku akijaribu kutoka kwenye maji, kila alivyojitahidi kutoka majini na wao walikuwa wanamfata wakimzonga na kumpatia vidonge vyake vya matusi makubwa makubwa, sauti zao zilikuwa zinapazika zinafika mbali, Lucky alisikia jinsi maryam anavyotukanwa na akaona alivyozongwa, alisimama na kujiuliza vipi akasogea karibu na maji yalipoishia, maryam nae alikuwa anakaribia maeneo hayo hayo tayari akiwa amefanikiwa kutoka majini.

" Hey guys vipi?. Aliuliza lucky.

" Vipi kivipi ndugu yako huyu?. Alisema kijeuri kijana mmoja.

" Nimeuliza vipi na wewe unantupia swali, mbona mnamzonga mwenzenu?. Aliuliza tena lucky.

" Huyu dem hana akili, tunamfata kwenda kuoga nae mtoto mzuri tupeane kampani anajifanya ni mzuri saaaaaana eti anakataa, tunamshika kidogo anatutukana tumemmaind sana haloo!. na wewe kama ni ndugu yake kaa mbali na sisi laa sivyo tunakushambulia na wewe sawa?. Alisema moja ya vijana hao lucky akaachia tabasam.

" Naombeni msimguse huyo mdada!, kama mna ubavu mnajiweza na nyie vidume kweli mnajiamini niguseni mimi. Alisema kwa kujiamini Lucky, maryam aliekuwa katika wakati mgumu alishangazwa na maneno ya lucky, vijana walionekana wameshiba wameshindikana lakini alisema nao kwa kujiamini.

" Mmemwelewa nyie huyu dem?. Alisema kijana mmoja aliejulikana kwa jina la Pita.

" Kwa iyo unaitaji uchezewe wewe au vipi. Alisema mwengine Seif.


Kutokana na walichoambiwa na lucky ikiwa vidume kweli wamguse yeye na sii maryam, walimsogelea na kuanza kumzunguka huku wakiamuangalia kwa dharau, seif alimshika kiuno chake pita akamshika shavu, hapo hapo lucky aliwachenjia na kuanza kuwacharaza makofi ya kushtukiza.

waliona wameshindikana ila lucky alishindikana zaid, makofi yaliwaingia wakatumia wingi wao kuitaji kumshushia kipondo, bahati mbaya au nzuri hawakufanikiwa kwa hilo kutokana na utata aliokuwa nao Lucky, mwili ulikuwa ni wa kike tena umekaa kirembo, ila roho yake na misuli yake ilikuwa zaid ya mwanaume, kupigana na kiumbe kinachoitwa mwanaume hakuona tabu, pengine kuna wanaume aliwazidi nguvu za mikono.


Vijana walipoona mziki wa bibie hawauwezi, wakiendelea kuwepo watarudi makwao na alama, waliamua kutoa mbio wakiamini ndo kitu pekee cha kuwaokoa kwa kuwa haziuzwi, walichanganya miguu bila kuangalia nyuma, walifika sehemu wakachukua nguo zao na kuchanganya tena mbariga, walipofika mbele ndo walikaa sehemu wakaanza kusimliana kilichowatokea, kila mmoja alimweleza mwenzake maumivu anayojisikia.

" Haijawai kunitokea. Alisema seif.

" Kaka kuna wanawake wengine hawafai.

" Yani yale makofi aliyonicharaza nimehisi napigwa na izrael. Alisema Pita.

" Katika maisha yangu nlisema haitokuja kutokea nipigwe na dem ila leo nimekiona chamtema kuni.

" Na pale tusingechanganya mbariga alikuwa anatutoa alama..


Lucky na maryam nao walipoona vijana wameondoka walitoka beach huku lucky akimpatia pole maryam, kulikuwa hakuogeki tena furaha ya beach iliondoka, maryam alimwangalia lucky kwa jicho la tatu na kujiuliza ni msichana wa aina gani.

" Mh!, kweli wasichana tunatofautiana, wengine tunawaogopa wanaume wakitusogelea tu tumekimbia lakini wenzetu wanawateremshia kipondo duh. yani nkiwa na lucky hata saa tisa natembea bila woga, hakuna mambo ya kukerwa kerwa anapiga kama mwanaume!?. Alijisemea moyoni mwake, alienda mpaka sehemu za kuoga akaoga maji ya kawaida, alipomaliza alivaa nguo zake wakatoka beach, jua la jioni ndo lilikuwa linaishia, waliingia ndani ya gari wakainza safari ya kuelekea kwengine, kwa kuwa usiku ulishaanza kuingia maryam hakuitaji waelekee chuo kwanza, badala yake walienda mpaka maeneo ya sinza kulikokuwa na sehemu nzuri ya kupumzikia na dina nzuri, ili wapumzike kwenye mida ya saa mbili na nusu au saa tatu waanze safari ya kuelekea mlimani..


Alihakikisha anampeleka lucky sehemu ambazo zitamfanya kufurahi na kuinjoy, na kweli lucky alionekana kufurahi sana baada ya kuingia sehemu iliyokuwa finyu ya faragha, alikuwa hajawai kushuhudia kicheko chake lakini lucky kuna baadhi ya mambo aliyaona huku wakiongea na kumpelekea kucheka, waliinjoy sana maryam hakujuta kumtoa lucky out kwani hakumuangusha, maeneo hayo kulikuwa na burudani za muziki zinaendelea na wasanii wa mambo ya kuchekesha, vitu vilivyowafanya wachelewe kutoka, saa tatu waliyokuwa wameipanga hatimae ilikuwa saa tano, saa tano na nusu ndo walitoka na kuianza safari ya kuelekea chuo, kwa muda ulivyokuwa umeenda maryam hakuona umuhimu wa kurudisha gari nyumbani.

saa sita kamili usiku waliingia katika geti la chuo wakakutana na magari kibao ya wanafunzi yakiwa yanatoka kwa sababu ya mambo ya weekend, walifika paking wakapaki gari lao wakafanya malipo ya ulinzi kisha kuitafuta njia ya kuelekea bwenini, ambayo waliifatisha ili iwafikishe room kulikokuwa na makazi yao..

" Nimefurahi sana leo, kiukweli sikutegemea kama itakuwa hivi, nakushukuru sana kwa kunifanya nijihisi mtu katika watu. Alisema lucky wakiwa wanatembea kidogo kidogo.

" mimi ndo nimefurahi zaid lucky.

" Kwa nini?.

" Ntakuambia kesho tukitoka class.

" Ok poa, Kesho una kipindi asubuhi sio?.

" Yah alafu tuko na profesa malki sasa.

" napenda sana masomo yake yule mzee.

"Ana elim ya saikology kichwani so anapofundisha lazima umpende tu, anacheza sana na vichwa vya watu.

" nakubali kwa hilo kwa sababu dah, huwa akiingia class kwetu moyoni hujihisi kupata furaha, nlivyochoka sasa yani nkifika ndani najimwagia maji nalala.

" Hatuna tofauti, nahisi mwili mzima hapa nlipo umezungukwa na kitu kizito.


Walipiga hatua moja baada ya nyingine wakiendelea na mazungumzo, waliingia kwenye majengo ya mabweni, waliambiana kiasi gani wamefurahi katika out yao, hasa lucky ambae alikuwa ana siku nyingi sana hajatoka, walipofika ndani waliingia kuoga kisha kupumzika, hawakuitaji kufanya lolote kwa muda huo, lucky alikuwa amechoka zaid ya sana, ilikuwa ni muda mrefu hajafanya mazoezi ya mwili, kila kiungo alihisi kinawaka moto, kitu kilichomfanya aitaji mapumziko ya muda mrefu ili kuwa sawa.


Hakuna kilichoendelea kwa usiku huo zaid ya usingizi, kipindi lucky anautafuta usingizi maryam yeye aliendelea kuwaza baadhi ya mambo aliyoyashuhudia kwa lucky.

" Kesho nkitoka class inabidi niende nyumbani kuongea na mama anambie kuhusu mzee edwad nimjue, uenda ndo mzazi wa Lucky.

Alijisemea moyoni mwake akavuta shuka kwa ajili ya kuanza kuutafuta usingizi, hadi kufika saa saba hakuna aliekuwa macho, Amina na tunu wao hawakuwepo, walikuwa wameenda sehemu za starehe kuisindikiza weekend, hawakuwa na mchezo na siku hiyo kwa kuwa nafasi yenyewe kuipata ni mara moja kwa wiki, siku nyingine zote wanakuwa bize na masomo..



Asubuhi na mapema wanafunzi wote wa chuo hicho kikuu dar es salam waliokuwa na vipindi asubuhi akiwemo maryam tayari walikuwa madarasani kuwasubiri walimu waje kuwapatia kile kilichowaweka chuo, hali ya hewa ilikuwa safi hasa maeneo hayo ya chuo, walipata nafasi ya kusoma vizuri kiubarid cha chini kikipenya madarasani. vipindi vilipoisha maryam ndo alikuwa wa kwanza kutoka akiwahi kwenda kufanya mambo yake mengine, kwa muda huo alikuwa anawaza sana kuhusu lucky kuliko hata masomo yake, hakuitaji kumtenga na kumnyanyapaa kutokana na alivyo kama walivyofanya wenzake, alitaka kufanya juu chini hata pesa kutumia kuhakikisha anajua kinachomsumbua na ikiwezekana amrudishe katika hali yake ya kawaida..

" Lazima nikupiganie Lucky my friend, nlikosea mwanzo nlipofurahi kuona huna furaha ila nimejifunza kutokana nawe na kuona kuna vitu vingi unavikosa. Nakupenda rafiki yangu. Alisema moyoni kipindi anatembea.


Akiwa katika mkusanyiko wa mawazo kuhusu lucky mwanadada alietokea kumuweka akilini kutokana na hali yake, alisikia sauti inamuita ikitokea nyuma iliyomfanya asimame ageuke kuangalia nani anamuita, alishangaa sana kumuona denis kijana ambae jana ya siku hiyo amepewa kipondo cha ukweli na Lucky, alijiuliza anataka nini kutoka kwake au ndo anataka kumpiga yeye ili amalize hasira za kupigwa na lacky.

" I'm Sorry Lucky, nadhani nimekushtua sana kukusimamisha bila kukuambia kama ntakuwa na mazungumzo yoyote na wewe. Alisema denis kumwambia maryam baada ya kufika karibu nae, jina lucky lilimshangaza bibie huyo kwani hakuwa yeye, kwa jinsi deniss alivyokuwa amechanganyikiwa hakufahamu kama anaeongea nae ni maryam hadi kumtamka Lucky.

" Mimi sio lucky deniss umechanganyikiwa?. Aliuliza maryam.

" Ooh God, okey i'm sorry maryam, Lucky yuko wapi?.


ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

BLOG