Search This Blog

Saturday, February 26, 2022

SIHITAJI KURUDI NILIKOTOKA - 1

  

IMEANDIKWA NA : SEID BIN SALIM 

********************************************************************************

Simulizi : Sihitaji Kurudi Nilikotoka 

Sehemu Ya Kwanza (1)


Mwaka mmoja ukiwa umepita tokea binti mwenye umri wa miaka 24 lucky ajiunge na chuo kikuu cha dar es salam UNIVERSITY OF DAR ES SALAM. Marafiki zake aliokuwa anakaa nao chumba kimoja katika hostel waliojulikana kwa majina ya Mariam, Tunu, na amina. Asubuhi na mapema ya wiki end waliamua kumkalisha chini rafiki yao huyo kwa ajili ya kuongea nae mambo flan, kutokana na jinsi walivyokuwa wanaishi nae katika hali ya unyonge na kuonekana hapend kushirikiana na mtu yoyote kimasomo hd starehe za hapa na pale.

waliishi nae kama sio mwenzao, walipoitaji ushirikiano wake hakuitaji kuwa nao, muda mwingine walimshuhudia akikaa kiupweke hadi kutoa machozi kwa muonekano wa kuwaza mambo mazito aliyonayo moyoni mwake, walimuonea huruma hasa kwa sababu wao ni watu waongeaji, walimkalia vikao vya kimya kimya walipopata nafasi ya kipeke yao, lakini namna siku zilivyozidi kwenda ndivyo lucky alizidi kutia huruma na kuishi katika mazingira ya kuusononesha uso wake, uvumilivu uliwashinda na kuamua kumkalisha chini ikiwezekana awaambie chochote kinachomsumbua moyoni mwake uenda wakawa na ushauri wa kumshauri.


" Lucky mpenzi, kikao hichi ni kwa ajili yako, tumeacha shughuli zetu ili tuongee nawe, tumeishi hapa mwaka sasa, lakini mwendo wako na wetu ni vitu viwili tofauti, kuna muda tumekushuhudia ukimwaga machozi bila sababu, mawazo yasiyoisha, huzuni wasi wasi na vingine kama hivyo, kitu ambacho kimetushinda kiukweli, kwa sababu sisi wakati wote ni watu wa kufurahi, kucheka, kununa kukasirika hatujui. so tunaumia sana tunapoona mwenzetu tunaeishi nae chumba kimoja hauko kama sisi, huoneshi furaha hata siku moja, tunaomba utueleze kitu gani hasa kinasumbua maishani mwako tafadhali.. Tunu aliekuwa pembeni yake alimuuliza akiwa amemuangalia kwa kushika mkono kwenye tama, lucky mwenyewe alishikilia mto uliokuwa mapajani mwake, machoni akionesha hayuko nao, mariam na Amina walikuwa wamekaa katika kitanda cha pili wakimtizama kwa macho yasiyoisha huruma.

" tunaomba utuambie kitu gani kinakusumbua maishani mwako, sisi ni marafiki wema, au tokea uingie hapa kuna jambo lolote baya tumekufanyia linalokufanya uwe hivyo?. Aliuliza Tunu lucky akatingisha kichwa kuashiria hamna. sasa kwa nini unatufanyia hivyo hatupendi lucky, twambie nini kinakusumbua hatuitaji uwe katika hali hiyo.

" Hapana Tunu mimi sina tatizo lolote. Alisema baada ya kupitisha mkono machoni kutoa machozi yaliyokuwa tayari yanamlenga.

" Lucky unajaribu kuficha ugonjwa usiofichika, hapo tu tayari machozi yanakutoka kisha unasema huna tatizo, tuko wanne tu hapa, zaid yetu hakuna mwengine anaetuona wala kutusikia tuambie tafadhali.. alisema dada mwingine Mariam ambae walipendelea sana kumuita Baby Mimah.

" mtoto koma mwengine yupo anaetusikia. Amina Alidakia maneno ya mimah.

" Ushaanza nani anatuona hapa?. Aliuliza mimah kwa kushtuka, amina kidogo alikuwa shambenga asietaka kitu kimpite.

" Sir God, anaona hadi uvunguni kama hujui.

" nlijua tu utasema hivyo, usilete matani wakati tuko serious bhna, unaichukulia baridi hali ya mwenzetu eee?

" Hapana kazi na dawa, kucheka kidogo kununa kidogo maisha yanaenda, bby lucky tunaomba utuambie basi kitu gani kinakusumbua mamy, ujue kukaa na tatizo moyono si kutatua tatizo ee. Alisema Amina.

" Sina tatizo mimi Amina niko kawaida.

" tatizo unalo, ujue hapa chuoni kuna kamchezo kabaya kanaendelea japo kwa upande mwengine kazuri, tukikuona hivyo hatukuelewi tutaenda kushtaki kwa calacte., so bora utuambie sisi mpenzi umbea utabaki humu humu ndani. Alisema amina huku akiwa amewaangalia wenzake.

" nawaomba hali yangu msimwambie mtu yoyote, siitaji watu wajue nnavyoishi, haya ndo maisha yangu tokea niko nyumbani. Alisema lucky akiwa ameangalia chini, waliendelea kumshawishi ili awaambie kile walichokuwa wanakiisi tokea kwake lakini wapi, mwisho waliamua kuachana nae wakimsihi sana abadilike laa sivyo watashindwa kuishi nae, upweke anaoweka hawauwezi kutokana na jinsi walivyozoea kucheka na kila mmoja..


Siku zilisonga mbele maisha ya lucky yakiwa hayo hayo ya ukimya muonekano wa msongamano wa mawazo na kujipwekesha na wenzake, ilifika sehemu wenzie anaolala nao walichoka ikabidi wamfate tena kumuweka chini lakini hakuna kilichobadilika, jinsi alivyokuwa anakaa alifanana na msaka tonge anaesaka tonge lake katika wakati mgumu wakati anatoka moja ya familia za kitajiri mno jijini DAR ES SALAM..

alivyoishi chuoni hapo lucky ( UNIVARSITY OF DAR ES SALAM ) walimu wengi walitokea kumpenda na kumjumlisha ndani ya daftari la wanafunzi bora mfano wa kuigwa na kila mmoja, kipindi chote cha mwaka mzima alibahatika kupokea tuzo ya mwanafunzi msafi na mwenye nidhamu kuliko wote, hakuna alichoambiwa na walimu afanye akakataa labda kiwe kibaya, alikuwa mtiifu kuliko watiifu, upole huruma kwa wanafunzi wenziwe pamoja na muonekano wa kudel na masomo wakati wote hata alipokuwa chumbani.

wengi walipendelea mambo ya michezo wanapokuwa hawana ratiba yoyote ya masomo, au kutumia muda huo kwenda kula bata sehemu mbali mbali maclub na kwengine, lakini yeye vitabu vilimkoma baadhi ya wanafunzi wakawa wanamuonea wivu, tabasam kwake ndo kilikuwa kicheko tofauti na wengine, hakuna alichokiitaji zaidi ya kusoma, pale alipochoka alipanda kitandani kulala, lakini moja ya kawaida yake ambayo anaolala nao waliizoea, hawez kulala mpaka machozi ya mawazo yamtoke, kitu kilichopelekea waamini uenda alipitia kipindi kigumu cha maisha ndo maana analia kila wakati.


Hakuna alieweza kujua kama lucky anatoka kwenye familia ya kitajiri sana uenda kuliko wanafunzi wote chuoni hapo, hakuwa akijionesha kuwa kwao uwezo upo tena mkubwa, alionekana mwanafunzi wa kawaida kuanzia mavazi, misuko ya nywele na vitu alivyokuwa anatumia.

Familia yake yote ilikuwa ikiishi pembezoni mwa jiji la dar masaki karibu kabisa na bahari ya hindi, mama yake aliejulikana kwa jina la jenipha alikuwa mganga mkuu katika hospitali ya mhimbili, kaka yake anaemfata alikuwa mmiliki wa makampuni matatu ya usafirishaji madini kwenda nje, huku baba yake mzee edwad akiwa mfanyabiashara mkubwa wa kimataifa..

Utajiri wa familia hii ulikuwa mkubwa mno kuliko hata wa viongozi waliokuwa madarakani. Iliishi kwa upendo muda wote, majirani waliiangalia kwa jicho la tatu namna inavyoishi, waliyatamani maisha yao wanayooneshana wakiwa nje, kitu kilichokuwa tofauti kwa mama mwenye nyumba jenipha aliekuwa anaiona bora jana kuliko leo, ila haikuonekana hivyo kwa majirani kwa sababu waswahili walishasema USILOLIJUA NI SAWA NA USIKU WA KIZA..


Maisha ya chuo kwa lucky yalisonga mbele, maryam, Tunu na amina waliamua kumuacha kama alivyo wao wakaendelea na ya kwao, walimtoa thamani na kumuona mjinga asiejua kitu na uenda ametoka shamba ( kijijini) ndo maana anakuwa hachangamuki, ila lililokuwa moyoni mwake hakuna alieweza kulifahamu, na alikubali kuonekana mjinga mbele ya wanaojiona wajanja ili maisha yake yaweze kusonga mbele..


" Rafiki yangu namuonea huruma sana huyu mwenzetu, yani anaishi kama mtu wa kijijini kimandazi mandazi tu sijui yukojee,, msiiiiu. Asubuhi ya jumaa tatu lucky akiwa bafuni anakoga kujiandaa kuingia kwenye kipindi ambapo wao walishajiandaa, Tunu alisema na wenzake namna anavyomchukulia lucky kwa kipindi hicho mbali na nyuma alivyokuwa akimueshimu.


" Si bora mandazi hayachachi, ila Achana nae mshamba huyo, ukimuita haitiki, ukimsemesha anajibu shot, ukimuomba hiki mpaka atake, ana nini kwani hadi tumbembeleze bhana, uzuri wa kutuzidi hana, akituzidi sehemu nyingine tu lakini si face, tufanye yetu tumpoezee aishi kivyake. Alidakia amina.

" mi nlizani mnankalisha chini kusema vitu vya maana kumbe ni huyu chapati, achaneni nae bhana. Kila mmoja mzuri humu ndani na kila mtu nyodo anaziweza, ametunyodoa tumnyodoe, tena sasa hivi niwakupewa visa mpaka chumba akihame hiki. Twendeni class. Alidakia maryam.

" hhhhhmmmmm. Aliguna tunu, kumbe na wewe umo?. Walinyanyuka na kicheko kila mmoja akabeba mkoba wake na kwenda darasani. lacky alitoka bafuni akiwa na khanga moja mwilini akakaa kitandani na kujifuta futa maji, hakukaa dakika akanyanyuka na kusogea kwenye kioo kujiangalia mwili wake wote ulivyo. Alivuta mafuta aina ya lotion akajipaka baadhi ya sehemu za mwili wake, alipomaliza aliitoa khanga mwili ukabaki utupu kisha akavaa nguo za ndani zilizokuwa kwenye henga..

Alimaliza kwa nguo za chuo akabeba mkoba na kutoka ndani, hadi anafika darasan hakuna alieweza kumpa hi kwa sababu ya kusikojulikana sana na watu, kwa alivyokuwa anajiweka hakuna aliweza kumzoea kwani hata mbinu ya kumuingia haikuwepo, wapo wanaume waliojifanya midomo mirefu kutaka kuingiza mistari ya kumtongoza kutokana na uzuri wa mvuto aliokuwa nao kuanzia sura hadi maumbile, lakini walijikuta wanashindwa na kujionea aibu namna ambavyo lucky hakutaka upumbavu.




" hhhhhmmmmm. Aliguna tunu, kumbe na wewe umo?. Walinyanyuka na kicheko kila mmoja akabeba mkoba wake na kwenda darasani. lacky alitoka bafuni akiwa na khanga moja mwilini akakaa kitandani na kujifuta futa maji, hakukaa dakika akanyanyuka na kusogea kwenye kioo kujiangalia mwili wake wote ulivyo. Alivuta mafuta aina ya lotion akajipaka baadhi ya sehemu za mwili wake, alipomaliza aliitoa khanga mwili ukabaki utupu kisha akavaa nguo za ndani zilizokuwa kwenye henga..

Alimaliza kwa nguo za chuo akabeba mkoba na kutoka ndani, hadi anafika darasan hakuna alieweza kumpa hi kwa sababu ya kusikojulikana sana na watu, kwa alivyokuwa anajiweka hakuna aliweza kumzoea kwani hata mbinu ya kumuingia haikuwepo, wapo wanaume waliojifanya midomo mirefu kutaka kuingiza mistari ya kumtongoza kutokana na uzuri wa mvuto aliokuwa nao kuanzia sura hadi maumbile, lakini walijikuta wanashindwa na kujionea aibu namna ambavyo lucky hakutaka upumbavu..


Songa nayo


Masomo yalipoisha wanafunzi waliokuwa wanamaliza vipindi walitoka madarasani akiwemo mwenyewe lucky, mkoba wake ulikuwa begani bila kuongea na yoyote akashika njia ya kwenda kwenye chumba anachokaa, alisimama ghafla baada ya kusikia sauti ya kiume inamuita, aligeuka akakutana na sura ya moja ya wanaume ambao huwa wanamsumbua sana chuoni hapo kumuitaji kimapenzi.

" Samahani lucky kwa kukusimamisha.

" Bila samahani.

" Leo tumebahatika kutoka mapema darasani, vipi tunaweza kuwa pamoja lunch mchana?

" Hapana haiwezekani.

" Kwa nini lucky.

" Sina sababu ila haiwezekani.

" Hivi unajua kuwa wewe ni msichana mrembo ambae kila mwanaume hapa chuoni anakumezea mate?, ila sijawai kukuona ukiwa na mchanganyiko wa mtu yoyote Yule kuanzia wanawake wenzio mpaka wanaume kwa nini?

" Hiyo ni moja ya sehemu za maisha yangu, ndo style nlopanga kuishi, alafu usiishi kwa kukariri kuwa kila mwanamke alopewa uzuri lazima awe na mchanganyiko wa watu, uzuri wangu haumaanishi kuwa kila mmoja anaeniita niitike.

" Ok lucky, mi nkutakie siku njema ila ningeomba kupata japo namba yako ya cm, nadhani ntajiona mwenye bahati sana.

" Samahani Denis pia haiwezekani kupata no yangu.

" dah, ok poa good day


Lucky aligeuka na kuondoka zake huku nyuma akimuachia lawama nzito kijana aliejulikana kwa jina la denis namna alivyokuwa anatingisha mauno yake aliyojaaliwa na Mwenye Ezi Mungu, kijana huyo hakuweza kugeuka kirahisi hadi alipoona lucky ameishilizia ndo alianza kutembea, moyoni alikuwa na umivu kali la kukosa bahati ya kupata walau namba ya lucky msichana alievutiwa nae tokea anajiunga nae siku ya kwanza darasani.

Bibie alifika chumbani kwake akaweka begi kwenye kiti akajitupa kitandani, alilala chali macho yakawa juu na kuingia katika wingu zito la mawazo, dakika kumi mbele tayari alikuwa anabubujikwa na machozi ambayo hakufahamu yanatokea wapi, marafiki zake anao kaa nao waliingia kipindi hicho hicho bila yeye kusikia hata mlango ukifunguliwa, uenda kutokana na kuwa mbali kimawazo, tunu maryam na amina walisimama vizuri mlangoni kumwangalia kwa makini, walipoteza zaidi ya dakika nzima wakashuhudia jinsi anavyobubujikwa na machozi, huruma iliwaingia wakamsikitikia kisha kumsogelea taratibu, maryam alifika karibu nae akakaa pembeni yake na kumshika pajani, lucky alishtuka akawaangalia na kuanza kufuta machozi.

" why lucky why my dia, alisema maryam kwa uchungu, kwa nini unatufanya kama watoto lakini, kitu gani kinakusumbua moyoni mwako hadi sasa si utuambie jamani mbona unakuwa hivyo?. Aliuliza maryam.

" Hamna kitu maryam. Lucky aliongea shot akamuweka katika kipindi kigumu cha kumkatili moyo maryam.

" dah, mi ni rafiki yako lucky, nakuomba usinifanyie hivyo nakupenda, naumia sana nnapokuona katika hali hii, sema kama unaumwa tukupeleke hospitali mbona marafiki zako tunakupenda sana why wewe huoneshi upendo kwetu?. Aliongea kwa uchungu maryam lakini lucky hakuwa tayari kuongea chochote, maryam nae alianza kulia baada ya kuona ni kama vituko wanafanyiwa na binti huyo wanae ishi nae chumba kimoja bila ishara ya kuonesha kabisa kuwa nao, tunu aliingilia kati akamzuia maryam kulia, walichukuana wote watatu wakatoka nje, walisimama na kuanza kushauriana nini wafanye juu ya rafiki yao japo walishaamua kumtoa thamani ikiwa yeye haoneshi ushirikiano nao, ila hali waliyomkuta nayo ilibidi wabadili mawazo yao na kutafuta mbinu ya kumsaidia kumwondoa katika janga alilonalo.


" kiukweli hali ya lucky mi inanichanganya sana siwachifi, yani bora kuishi na nyoka ikawa inakudonyoa tu uenda maumivu yataisha kuliko kuishi na mtu wa aina hii Akyamungu. Alisema maryam.

" maryam unajiumiza kichwa tu my dia, hadi machozi yanakutoka kabisa kwa mtu kama huyo. Alisema amina.

" sijafundishwa hivyo mamy, roho yangu ni nyepesi sana nnapomuona mtu anateseka kwa kitu kisichojulikana.

" mimi nna wasi wasi lucky ametokea kwenye maisha ya shida sana, au hapa mjini ni mgeni maana kila kitu hajiwezi, story hawezi, kampani hakuna, kicheko kwake hakijawai kuonekana, kuongea na mwanaume hapana, sa si tumchukuliaje, ujue anazingua sana huyu dem. Alisema tunu.

" Anazingua anazingua!!!, ila nna wazo. Alisema Amina.

" wazo gani. Aliuliza maryam.

" twende tukapeleke malalamiko kwa msimamizi kiranja.

" Good, aidia nzuri sana hiyo, twende huko huko tumueleze kuwa mwenzetu hatumuelewi tumpe A to Z. alisema tunu.


Wazo hilo lilipita kwa wote wakatoka taratibu hadi sehemu alipokuwa msimamizi wa wanafunzi wote chuoni hapo, alikuwa mwanadada aitwae Sophia wakakaa chini na kuanza kumpa moja mbili tatu kuhusu lucky, lucky mwenyewe hakuwa anajua chochote wanachofanya watu anaoishi nao chumbani, alijipozea tu kitandani wimbi la mawazo likizid kumtafuna..

" Dada Sophia tumeishi na mwenzetu lucky mwaka sasa, lakini kwake hatujawai kuona kicheko, tabasam, furaha zaid ya huzuni, kilio kisichoisha, na ukimya basi, tunahisi atakuwa ana kitu kikubwa sana akilini mwake kinachompelekea kuwa hivyo, ila sasa hali yake inatutesa, kama kuna uwezekano mhamisheni hata chumba au kaa nae chini umsomeshe umpike akueleze kinachomsumbua au abadilike si hatuwezi kuwa na mtu wa aina ile, wee mtu kicheko tu kwake ni kama sikukuu, aka! sisi hatuwezi dada Sophia, pia tunamuonea huruma maana si usiku si mchana yeye na kilio ndo nini sasa?. Alisema amina akitumia zaid ya dakika kumi kuongea, kila kitu kilichokuwa kinaendelea kwa dada lucky alikiropoka mbele ya Sophia ili kuangalia kama uwezekano wa kutatua tatizo lake utakuwepo au laa.

" Mmekaa nae mwaka sasa katika hali hiyo kwa nini hamkufanya hivyo kipindi cha nyuma mfanye sasa?. Aliuliza Sophia baada ya kumsikiliza amina kwa makini.

" sa sisi tulikuwa tukimuangalia tu labda atabadilika lakini wapi. Alisema Amina.

" mmejaribu kumkalisha chini kumweleza?.

" ndio tena sii mara moja wala mara mbili.

" ok sawa nimewasikia ntalifanyia kazi.

" tena ukikaa nae mwambie kabisa tumechoka, wee jitu halijui hata kucheka bhna. Alidakia maryam akaongea kwa hasira.

" sawa nimewaelewa rudini chumbani kwenu. alisema Sophia kwa muonekano wa kuwa mkali kidogo, ila hawakushtuka ilikuwa kawaida yake, waliinuka kurudi chumbani kwao kabla ya kufika kokote tunu aligeuka.

" bora umwite sasa hivi uongee nae maana yuko analia huko chumbani.

" naomba mrudi kwenye room yenu tafadhali.


Hawakumuongelesha lengine walitoka wakatembea hatua kadhaa ambazo ziliwafikisha room, lucky tayari alikuwa ashamaliza kulia muda huo alikuwa amekaa kitandani anajisomea, pia hawakushangaa kwani ilikuwa moja ya kawaida zake, walipita kila mmoja akapanda kitandani kwake wakatoa cm zao na laptopz kwa ajili ya kuanza kuchart na kuperuzi katika mitandao mbali mbali.


Lucky aliwaangalia akatingisha kichwa na kwendelea kujisomea huku wao wakiwa wanachart, masaa yalisonga mbele siku ikaisha na kuingia siku nyingine, ilikuwa jumaa mosi kulikuwa hakuna anaeingia darasani, kila mmoja alichelewa kuamka isipokuwa lucky alieamka saa moja na kuingia katika dimbwi zito la mawazo, mlango uligongwa akashtuka na kujiuliza nani anawagongea mlango asubuhi yote hiyo wakati dada wa usafi huwa anaingia saa mbili na nusu. Uligongwa tena akaweka khanga yake vizuri aliyokuwa ameiegesha tu mwilini kisha kuinuka kitandani, alisogea hadi mlangoni akafungua na kuchungulia nani anagonga, macho yake yaligongana na macho ya Sophia kiongozi wa chuoni hapo, woga ulimuingia mapigo ya moyo yakaamka akamkaribisha huku moyoni akijiuliza mbona Sophia yuko hapo kwa muda huo.

" asante nshakaribia mambo? Alisema Sophia baada ya kukaribishwa.

" poa

" nimekuaribia usingizi wako ee, nsamehe mwaya!

" wala, nlishaamka zamani wala usijali kuhusu hilo.

" mapema yote hii.

" yah kuna masomo jana yalinichanganya ndo nlikuwa nayapitia, si unajua asubuhi kunakuwa hakujachanganya masomo yanaingia?.

" yah nalijua hilo, na wenzio vipi hao tayari au bado wameuchapa. Aliongea akiachia tabasam.

" wao bado wamelala.

" Ok poa, nakuomba ofisini kwangu mara moja basi nna maongezi na wewe samahani lakini. Alisema Sophia lucky akashangaa.




Songa nayo


" ofisini kwako?

" Yah

" um, kuna tatizo lolote?

" Hapana lucky, ni mambo ya kawaida naitaji tuongee.

" ok sawa nakuja. Alijibu akiwa na wasi wasi wa kuhisi uenda jamaa zake washapeleka malalamiko, Sophia alimuaga na kumuitaji asichelewe kisha akaondoka, lucky alirudishia mlango akasimama katikati mwa mlango na kuangalia vitanda walivyokuwa wamelala wenzake, alitembea taratibu mpaka bafuni ambako alitoa khanga yake na kubaki mtupu, aliachia maji akavuta sabuni, alitengeneza nywele zake zisije kuingia maji, alianza kujimwagia kidogo kidogo huku akilini akijiuliza maswali mengi ambayo hakuwa na majibu yake.

Alimaliza kuoga baada ya kutumia dakika tano hadi sita akiwa bafuni, alivaa nguo haraka haraka akatoka kuelekea ofisini kwa Sophia, akiwa njiani cm yake ilianza kuita, kuangalia kwenye screen alikutana na jina la baba yake, badala ya kupokea na kuwa na furaha kama wanafunzi wengi wa hostel wanapokuwa wanapata bahati ya kupokea cm toka nyumbani, aliikata na kuzima moja kwa moja sura yake nayo ikibadilika kutoka katika mwonekano wa kawaida hadi mwonekano wa chuki.


Alifika kwenye chumba cha Sophia akapita hadi ndani, Sophia aliacha kazi zake alizokuwa anazifanya ili aweze kuongea nae.

" karibu sana lucky.

" asante nshakaribia

" nimemaliza kupata kifungua kinywa umechelewa.

" wala usijali kuhusu hilo.

" Uhm mpenzi!, nimeletewa malalamiko hapa na wenzako, kuwa unavyoishi ni tofauti na wao kabisa kwa nini?. Aliuliza Sophia.

" nlijua tu unaniitia hilo mumy, kiufupi hayo ndo maisha yangu nliyoyachagua kuishi sophia, kila mmoja ana style yake inayomfaa katika maisha, maisha ya chuo nayajua nkianza kujichanganya sitosoma wakati naitaji kufika mbali. ili mradi simtukani mtu, sigombani na mtu, simjibu vibaya mtu, wana haki ya kuishi kivyao na mimi kivyangu, nkiamka nawasalimia, tukinunua chakula tunakula wote wakikosa pesa wakanambia nawapatia. furaha yangu ni kitabu madam mengine siyaitaji. Alisema lucky na kumuacha Sophia njia panda, hakujua ashike wapi aache wapi kwani maelezo yake yalikuwa majibu mazuri tosha, hakuwa na la kuongezea alimwambia amerizika na majibu yake, waliongea mambo mengine huku lucky akimsisitizia kwa kumwambia kuna watu wanapenda kujua binadam wenzao wanaishije ili wawapande kichwani lakini kwake hilo haliwezekani.


Sophia alimruhusu arudi chumbani kwake, dada huyo ni mwanamke aliekuwa na akili nyingi sana za kumtega mtu, kilichokuwa kichwani mwake baada ya kumruusu aondoke alikijua yeye, ila muda waliotumia kuongea na maongezi waliyoyazungumza na jinsi walivyokuwa wanaongea, alipata kufahamu kuna tatizo linamsumbua bidada lucky japo haitaji kulionesha.

" Unaonekana mpole na mtaratibu lucky ila una tatizo linakusumbua na mimi ntalifanyia kazi mpaka nlifahamu.. alisema peke yake.


Lucky alirudi chumbani akawakuta wenzake bado wamelala, aliwaamsha akawakalisha kitako kutaka kujua kitu gani kimewakuta hadi kwenda kwa Sophia kumweleza matatizo yake.

" Friends, nawaeshim na mimi naomba mnieshim, msione kwa kuwa nakaa kimya siongei mkajua ni mjinga na zoba kiiivo tafadhalini, kila mmoja ana maisha yake ya kuishi, na kila mtu hapa amekuja kwa pesa zake na akili zake, hivyo sitaki mniingilie kwenye maisha yangu, nkiwatukana nendeni mkaseme, lakini ili hali siwatukani siwadharau tafadhali tueshimiane, kama hamuitaji kuishi na mimi semeni na kama mnahisi nawanyima uhuru waambieni wawapatie chumba kingine mniache peke yangu kwa sababu uwezo wa kulipa chumba kizima hiki nnao, msitake kunipanda kichwani nawaombeni na nawaombeni tena, maisha yangu hamyajui niacheni kama nlivyo. Alisema kwa hasira.

" lakini lucky!, kitu gani sisi hapo tumekosea?. Tunaumia tunapoona unaishi kiunyonge mpenzi, usituchukulie vibaya unajiathiri kisaikolojia lucky. Alisema maryam.

" siitaji niacheni niaribike kisaikolojia, naishi nitakavyo na sii mtakavyo Hey!, kwani lazima?. Alisema lucky.

" Basi dada yaishe, tusamehe kwa kirehe rehe chetu cha kutoa kwaito zetu hapa hadi kwa Sophia. Alisema tunu.

" ila na sisi umbea umetuzidi una haki ya kutuchamba. Alidakia Amina.



ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

BLOG