Search This Blog

Saturday, February 26, 2022

SEKESEKE (ROHO MKONONI) - 2

   

Simulizi : Sekeseke (Roho Mkononi) 

Sehemu Ya Pili (2)


Palepale Butu akaanza kulia,SAM alikuwa na wakati mgumu sana kumuweka sawa ila mwisho alifanikiwa sasa akawa akipokea pole,akaenda kuiangalia familia yake,waandishi nao awakubaki nyuma kuripoti swala lile...magazeti ya mchana yakajaa habar hizo,televisheni zikarusha mubashara tukio lile wengi wakimpa pole,mkuu wa polisi IGP SULTAN BOZI akatoa ahadi ndani ya masaa 48 kuwatia mkononi wahusika wa tukio lile,baada ya uchunguzi inspekta akakabidhiwa maiti ya familia yake kuzizika...


Watu wengi akiwemo Raisi wa Jamhuri ya muungano walikwepo msiba ule ulitikisa taifa,baada ya mazishi inspekta Butu akala kiapo mbele ya makaburi ya familia yake,kuhakikisha anaua wote walohusika na vifo vya familia yake,tena atawaua kikatili,aliapa kutenda ivyo!


MASKINI!,KUMBE AKUJUA WALOFANYA IVYO NI WATU WA NAMNA GANI,AKUJUA FIKA!


Na laiti angejua?!,asingekuwa na mawazo ya kuwafatilia watu hao,ila ndo usilolijua ni sawa na usiku wa kiza!...




Inspekta wa jeshi la polisi John Butu anakula kiapo mbele ya makaburi ya familia yake kulipiza kisasi kwa kuwa angamiza wote walohusika katika kuiteketeza familia yake,mbaya zaidi akujua anaenda kupambana na watu wa aina gani!,ni vita inayohatarisha maisha yake ungana na mtunzi Zuberi Maruma uburudike na riwaya hii ilojaa upelelezi,na ujasusi ndani yake


HATUA YA SABA


SURA YA PILI


Inspekta Butu aliwasili ofisini akaweka saini mapokezi ile anaelekea ilipo ofisi yake ghafla akaitwa nyuma yake na sauti nyororo,


"Samahani afande mkuu kasema ukija kabla ujafanya chochote ukamuone"


Ilikuwa ni sauti ya askari mwenye cheo cha Konstebo alokuwa mapokezi muda huo!


"Sawa Fatma hiyo aina tabu!"


Butu akajibu na kugeuka kuelekea ilipo ofisi ya kamishna Nurdin Kyango.


Alifika akabisha hodi mara moja kabla ya kusikia sauti ya kukaribishwa akaingia na kupiga saluti mbele ya mkuu wake!


"Kwa niaba ya jeshi la polisi nikupe pole sana afande kwa yaliyokukuta ni ajali katika kulitumikia taifa lako,na barua hii...


Nurdin aliongea huku akimkabidhi Butu barua,Butu akaipokea na kuifungua palepale na kuanza kuisoma!


Alikuwa na maana yake kuisomea pale,na kama alijua barua ile ni ya kumpa likizo ya mapumziko ya mwezi mzima kusudi akili ikae sawa!


"Hapana mkuu,sipo tayari kwenda likizo nahitaji nishirikiane na mwenzangu kuchunguza juu ya walohusika na vifo vya familia yangu,kivipi nikae nyumbani hali ya kuwa wakatili wa familia yangu wanaishi nishahapa nitawaua wooote"


Butu aliongea kwa uchungu huku akiwa kakasirika.


Nurdin akatingisha kichwa,


"Butu wewe kuua ni kwenda kinyume na sheria,kwa sasa akili yako ijakaa sawa yakupasa ukapumzike,acha sisi tutalisimamia swala lako na wote walohusika tutawakamata na kuwapeleka mbele ya sheria wakapate adhabu inayostahili!,kwa sasa wewe upaswi kufanya chochote unaongozwa na hasira utadhuru hata wasousika..."


"Hapana mkuu,sitoweza kutulia bila kuwakamata makatili wangu!"


Palepale akageuka na kuufata mlango akaufungua na kutoka,huku nyuma Kamishna alishika mkonga wa simu na kumpigia


"Alooh mkuu Butu kakataa kwenda likizo,kahaidi kuisimamia kesi ya familia yake na yeyote atakayemgundua anamuua sijui tufanyaje mkuu!"


"Ok! Ahsante kwa kunijulisha wacha nimuandalie uhamisho ntampa kijana wangu alete"


"Ok mkuu!"


Nurdin aliitika na kukata simu,alishapoteza raha,ghafla akaingia kwenye mawazo!


Mawazo juu ya inspekta John Butu...


kivipi?!


***


Butu alitoka ofisini kwa bosi wake huku akiongea mwenyewe tena kwa kunung'unika,akiwa kakunja sura,ni baada ya kupewa barua ya likizo ya mwezi mmoja!


Katu akujua anaandaliwa barua ya uamisho,taratibu akaelekea zilipo mahabusu akafungua mlango


"Zuberi nakuhitaji"


Akaongea na kugeuka....


Mahabusu pale aliinamia magoti kijana mmoja , baada ya kusikia akiitwa akanyanyua uso wake macho yalovimba kwa kulia yakaonekana,kijana yule akanyanyuka na kumfata inspekta mpaka katika ofisi yake.


Huyu alitambulika kwa jina la Zuberi Maruma,alokamatwa siku chache zilizopita na Inspeka Jonathan,Ni baada ya Inspekta Butu siku ile kupigiwa simu na mtu asiye mjua akitumia namba 0759427653 na kumpa vitisho kwamba awaachie watu wake pamoja na mzigo wake wote tofauti na ivyo ataiteketeza familia yake, palepale Butu akaituma ile namba kwa Kpl 001 kitengo cha mawasiliano sambamba na kwa mkuu wake,kamishna Nurdin akamruhusu kwenda nyumbani kuicheki familia yake akihaidi kuchunguza zile namba,ndo pale Butu alipochukua pikipiki kuwahi kwake ambapo aliikuta familia yake aipo aka amua kurudi kituoni na kuwa achia wale watuhumiwa!...


Kamishna naye usiku ule alimpigia kpl 001 kitengo cha mawasiliano kuomba taharifa za namba hiyo!


"Usajili wa namba hizi jina ni la Zuberi Maruma,mkazi wa hapa hapa jijini dar anapatikana maeneo ya temeke maghorofani block 2 ana miaka 35 kazaliwa tarehe 15 mwez wa pili mwaka..."


"Inatosha..."


Nurdin akamkatiza,usiku ule ule kamishna akampigia simu Jonathan na kumpatia kazi ya kwenda kumkamata Zuberi kweli Jona na askari kadhaa usiku ule ule wakaingia katika kitara mpaka walipoelekezwa,wakamkamata huyo kijana na kumpeleka kituoni.


Akaswekwa ndani.


Kabla ajaojiwa ghafla Butu aliwasili usiku ule na kuwatoa wale vijana watano!.


Ndivyo ilivyokuwa.


Ivyo wakati wa msiba na uchunguzi wa miili Zuber alibaki ndani pasina kuulizwa chochote!,mpaka siku hii Butu akiwa na hasira akaenda kumtoa na kumswaga mpaka katika ofisi yake.


Akampa ishara aketi mtu yule akaketi.


Butu akamwangalia kwa dakika kadhaa na kumtathimini,moyoni mwake alijikuta akikataa kuwa yule si alokuwa akiongea naye kwenye simu,mwenye sauti ya majivuni!,mmiliki wa vijana wa madawa ya kulevya alowakamata uwanja wa ndege!.


Sasa huyu ni na nani?!,na namba zilizo mpigia inasemekana mmiliki Ni mtu huyu?!,akatafakari na kujiuliza maswali

Mwisho akaona asijiumize kwa maswali wakati mwenye majibu yupo mbele yake.


"Unaitwa nani bwana mdogo?!"


Akaanza kuhoji huku macho yake yakiwa usoni kwa mtu yule.


"Zuberi Maruma"


Mtu yule akaitikia,Butu akatabasamu,na kuandika jina lile katika kakijitabu chake.


"Una miaka mingapi Zuberi?!"


Inspekta akauliza kirafiki tu


"Thalathini na mbili!"


"Ok umeoa"


"Hapana"


"Unaishi na nani?!"


"Naishi mwenyewe"


"Umepanga"


"Hapana nimejenga"


"Wafanya kazi gani!?"


"Mwandishi wa Riwaya"


"Nyumbani unapokaa unaishi na nani?!"


"Afande nishakwambia naishi mwenyewe"


"Kwa nini?!"


"ah afande ungetaka niishi na nani?!"


"Mpaka miaka yote hiyo ujaoa wasubiri nini?!"


"Ni mipango yangu binafsi"


"Ok siku ya tukio ilikuwaje?!"


"Nikiwa nyumbani kwangu mida ya saa tatu usiku Askari walikuja na kuniweka chini ya ulinzi wakanileta hapa kituoni"


"Ulijua kosa lako?!"


"Hapana sikujua na Wala sija ambiwa"


"Uliuliza?!"


"Ndiyo,ila sija ambiwa"


"Nawe una hisi unakosa gani?!"


"Sijui"


"Kwa nini ujui?!"


"Kwa kuwa Sina kosa lolote!"


"Kwa hiyo wahisi umekamatwa bure?!"


"Inawezekana"


"Ok hii ni simu yako?!"


"Ndiyo ni simu yangu"


"Unaweza nitajia namba ya line zilizopo humu ndani"


"Tigo 0673999120 na voda 0759427653"


Inspekta Butu akaguna kidogo baada ya kusikia zile namba za voda,ni zile zile za yule mnasibu wake aloiteketeza familia yake...


"Simu yako unaitumia na nani?!"


"Peke yangu"


"Siku za karibuni ushamwachia mtu?!,au kumpa yeyote line yako?!"


"Hapana!"


Butu kuhakikisha akaingia upande wa meseji katika ile simu ila akukuta sms ilomuhusu akaenda upande wa simu zilizopigwa akatafuta namba yake ila akuzikuta,upande wa simu zilizo ongelewa pia akuzikuta.


Ina maana zimefutwa?!,akawaza pasina kupata jibu,akarudi katika simu yake na kutafuta sms ya mwisho kutumiwa akaikuta,akapiga zile namba simu ile ya Zuberi ikaita hii ikiwa na maana namba Ni zilezile akamgeukia tena Zuber sasa akiwa kakunja uso akarudia swali lake la awali!.


"Simu yako unatumia na nani,au nani ushampa simu siku hizi za karibuni?!"


Sasa alikuwa akimsogelea pale alipokaa!


"Hakuna afande huwa natumia mwenye..."


Paaaaaaaaaaaaaaaaaa


Kibao kikali kikatua shavuni kwa Zuberi,meno matatu palepale yakaacha fizi mdomo ukajaa damu.


Butu sasa alishabadilika,mishipa ya kichwa ilimsimama alidhamiria kuua kama kijana yule asingemweleza ukweli alijua lazima kijana yule hatakuwa anamjua yule alokuwa akimpigia kwa namba zile ila hakutaka kujidanganya Zuberi ndo alokuwa akiongea naye,hili alikataa kabisa.


Usilolijua....


*BUTU ANA ANDALIWA UAMISHO!,ATAKUBALI KUONDOKA PASINA KUWAPATA WABAYA WAKE?!*


*ZUBERI NAMBA ZAKE NDIZO ZILIZOKUWA ZIKITUMIWA NA MTU ANAYEMSUMBUA BUTU,JE WANA UHUSIANO GANI AU ZUBE ANAMJUA MTU HUYO NA ATAMWELEZA UKWELI BUTU?! NA NI NANI MTU HUYO?! NA NI KWA NINI ATUMIE NAMBA ZA ZUBERI?!*


Mambo bado mazito tuonane katika hatua ijayo kwa mwendelezo..


Inspekta wa jeshi la polisi John Butu bado anaendelea na upelelezi mkali kumjua muhusika wa mauaji ya familia yake,na sasa kafanikiwa kumpata mmiliki wa namba za simu zilizokuwa zikitumiwa na mtu huyo alo msevu kwa jina la 'mr x' katika simu yake,


Moyoni mwake anakataa kwamba mtu yule 'Zuberi' siyo lakini ndo mwenye namba,anaanza kumtesa vikali akitaka kujua ni nani alompa namba yake aitumie,je Zuberi atamtaja?!,na kama si yeye ni nani mtu huyo?!


TUSONGE KATIKA:


HATUA YA NANE


Inspekta Butu akamkwida Zuberi shati! na kuanza kumfokea kwa ukali:


"Kwa hiyo utaki kunieleza siyo?,unatumiwa eeh! Utanieleza tu!"


Palepale akarusha ngumi palepale mdomoni,Zuberi akaachia yowe,


"Sijampa mtu afande unanionea bure!"


"Sasa alotuma hii meseji ni nani?,si namba yako hii au?!"


Palepale akamkabidhi Zuberi simu yake,


"Ongera afande kwa kujiokoa,ila je utaweza kuiko mboa familia yako?! Nakupa dakika kumi na tano uchague kuikosa familia yako? Au kuwa achia watu wangu nawe kuipata familia yako maamuz juu yako"


Zuberi akamaliza kusoma sms ile kutazama jina lililoseviwa ni "Mr x" kucheki namba alishtuka!


Zilikuwa ni namba zake za voda,


Mikono iloshika ile simu ikaanza kutetemeka,meno mdomoni yakaanza kugongana yenyewe.


"Hizo si ndo namba zako na ujawah mpa mtu simu je hii meseji ulo ntumia ilikuwa na maana gani?!"


"Hapana afande,siyo miye nilokutumia"


"Ndo unieleze ndo nani sasa ulo mpa simu yako akantumia mie meseji tofauti na ivyo utaya beba madhambi yake unajua alochoifanyia familia yangu?,utamtaja tu huyo kibaraka wako"


Butu aliongea kwa hasira huku akikunja mikono mirefu ya shati lake! Kilichofatia ni kipigo kikali,kipigo kilichoisha baada ya Zuberi kupoteza fahamu,askari wakaitwa wakambeba kijana yule na kumrejesha mahabusu,wakamweka huku akiwa vilevile kapoteza fahamu!


'Huyu lazima atakuwa naye ni kibaraka wa yule shetani sina haja ya kumuacha hai usiku wa leo atanieleza akizidi kuwa msiri sitosita kumchinjilia mbali"


Butu akawaza,tayari alishavaa roho ya kikatili, yeyote ambaye alihisi kwa namna moja ama nyingine anahusika na vifo vya familia yake alishahapa kumteketeza,na leo alipanga kuanza na Zuberi,ushahidi ukiwa ni namba ile!...


Maskini Butu akujua kuwa anaenda kuua kiumbe kisicho na hatia...


Ilipofika mida za saa moja za usiku akiwa na baadhi ya maaskari wenzake wakamtoa Zuberi mpaka ndani ya gari yao wakaelekea naye mpaka katikati ya msitu Tasa,palepale alipoikuta miili ya familia yake!,wakamshusha na kuanza kumtesa vikali kijana yule,wakimlazimisha aeleze ukweli,ila ukweli ni kwamba Zuberi akujua chochote kuhusu kutumika kwa namba zake,je angeeleza ukweli upi?!


Butu akamuona kijana yule ni kiburi,'Kama nilivyohaidi kumuua yeyote ambaye anausika na vifo vya familia yangu naanza na wewe,japo ujataka kunifungulia njia sawa kawafungulie wenzako njia soon watakufata mpuuzi wewe!'


Butu aliwaza huku akiwa kakunja sura na palepale akapayuka...


"Tunakupa muda wa kujitetea haya kimbia..."


Maskini pasina kujua Kwa shida Zuberi akaanza kukimbia risasi kadhaa zikaushambulia mgongo wake,nyingine zikikishambulia kisogo,wakaubeba ule mwili na kurudi nao kituoni!


Kesho yake habari zikatapakaa katika vyombo vya habari,jambazi lauwawa wakati akijaribu kukimbia mahabusu,ni yule mwandishi mahiri wa vitabu mtandaoni,kila gazeti lilikuja na habari yake,kwa majonzi familia ikachukua mwili wa marehemu na kwenda kuuzika.


OFISINI KWA KAMISHINA


Kamishna Nurdin alionekana wazi kuchukia,mbele yake alikwepo inspekta Butu!


"Najua wewe na wenzako ndiyo mlousika na mauaji ya yule mshtakiwa!"


"Ilibidi nifanye ivyo mkuu,sioni faida ya kukaa na mtu ambaye atoi msaada wa nini sasa?!"


"Ndo umuue?!,wakati unajua yule alikuwa ndo mtuhumiwa pekee ambaye angewezesha kukamatwa kwa wahusika we unaenda kumuua utawajibika kwa hili afande"


"Niliapa kumuua yeyote ntakayegundua kwa namna moja au nyingine ni mshirika wa yule alosababisha niikose familia yangu,huyu kijana namba zake ndizo zilizotumiwa na adui yangu naye kamficha sijui ndo kibaraka wake au vipi!,kifo kilikuwa ni haki yake!"


Kamishna hakuwa na la kuzungumza zaidi,kikubwa alisubiria barua ya uamisho ya kijana huyo ifike katika meza yake mtu yule aondoke,hakukuwa na msaada mwingine zaidi ya huo akampa ishara Butu atoke!


Butu akapiga saluti,na kugeuka kwa hatua zake ndefu akaufikia mlango akaufungua na kutoka...


Wakati akiwa katika korido moja ndefu akipita ofisi mbalimbali ghafla simu yake ikaita,haraka akaingiza mkono mfukoni kuitoa!


Namba alizokutana nazo ilibakia robo,simu ingemponyoka na kwenda chini,ila akawahi kuukaza mkono,


"MR X"


Ndo jina alilolisoma katika kioo cha simu yake,chini ya jina lile pakiwa na zile zile namba 0759427653 haraka kwa uwoga akapokea ile simu...


Ni sauti ile ile nzito,ilo msaliti na kumuulia familia yake hata baada ya kuwaachia watu wake na mzigo wake wote "ha ha ha ha pole sana askari kwa misiba ilokupata,pia nasikia umeua kiumbe kisicho na hatia kisa tu kumshukia na yeye kutumia namba kama zangu ukasahau kabisa kuwa kuna ku ack namba,pili binafsi nisingeweza kukupigia kwa kukutumia namba zangu hivyo nikafanya mautundu yangu nika ziunganisha hizo namba nanyi bila kufikiria mkamkamata mtoto wa watu na mwisho kumuua kwa akili zako ndogo ulijua kijana mdogo kama yule ataweza miliki mzogo wote uloukamata?!,kwa maisha yale ya kale ka jumba cha vyumba viwili?!,apumzike kwa amani,hili silo lililonifanya nikakupigia,nasikia eti wantafuta ok usijali nakupa nafasi ya kuonana na Mimi leo saa tatu usiku katika Bar ya Kivulini,uje mwenyewe asante....


Palepale simu ikakata


Butu alibaki kaduwaa,akuamini kile alichokisikia kwanza alishtushwa na mawili cha kwanza kumuua kijana wa watu asiye na hatia ,kilicho mshangaza Ni kitendo cha Mr x kuhitaji kuonana naye usiku katika Bar ya kivulini.


Je Ni mtego gani aloandaliwa akajikuta uwoga ukimvaa ila itakavyokuwa na iwe akaapa usiku aelekee kivulini akakutane na huyo mtu!


"Amuue yeye au afe yeye..."



Butu alibaki kaduwaa,akuamini kile alichokisikia kwanza alishtushwa na mawili cha kwanza kumuua kijana wa watu asiye na hatia ,kilicho mshangaza Ni kitendo cha Mr x kuhitaji kuonana naye usiku katika Bar ya kivulini.


Je Ni mtego gani aloandaliwa?!


Akajikuta uwoga ukimvaa ila itakavyokuwa na iwe akaapa usiku aelekee kivulini akakutane na huyo mtu!


"Amuue yeye au afe yeye..."


HATUA YA TISA....


Baada ya mtu yule kukata simu,Butu akaingia katika tanuri la mawazo,moyo wake ukayavaa majuto makubwa kwa kile alichokifanya,akajilaumu kwa kutojipa muda wa kutafakari hapo awali,akili yake akaiendesha kwa hasira mpaka kumuua mtu asiyehusika!.


Na sasa muhusika wake anahitaji waonane,anajiaminije?!,lipi lengo lake kwake?,je arejee ofisini kwa bosi wake kamishna akamueleze kuwa ile namba imempigia tena na wakati huu imemuomba waonane?!


Hapana!


Akapingana na wazo hilo baada ya kugundua kuwa atazalisha lawama nyingi ikiwa mkuu wake atagundua kamuua kiumbe asiye na hatia!.


na anaweza pia kushtakiwa!...


Akazikumbuka lawama alizotoka kuzipokea muda mchache ulopita,hapo mkuu wake alijua yule ni mmoja wa walohusika,je sasa akagundua kijana yule mwandishi wa hadithi akuhusika ila ni namba tu zili akiwa?!...


Hapana!,akaona aifai ibaki siri yake naye aendeleze upelelezi wake wa chini kwa chini!


Akaelekea mpaka mapokezi,akahitaji maaskari watatu wa kiume kwa maongezi maalumu!.


Dakika kadhaa zilizofatia watu wa nne walikwepo ndani ya chumba kidogo cha ofisi yake


"Ma afande nyinyi mkiwa kama watu wangu wa karibu,wasiri wangu nadhani mengi tumefanya tukiwa pamoja,kwa taharifa tu yule mtu tulomuua msitu Tasa hakuwa na hatia!"


"What?!" Askari wale wote wa kashtuka,hakuna kitu askari anacho ogopa au kukijutia kama kuhukumu kiumbe kisicho na hatia achia mbali kuua,


Ikabidi Butu awaeleze ukweli wote juu ya simu ile alopigiwa na kuchekwa kupewa maneno ya kejeli! Na mwisho mtu yule kuhitaji kuonana nae!,watu wale wakashtuka!...


"Muonane kirahisi tu?!" Inspekta Jona akauliza,huku wasiwasi ukionekana wazi usoni mwake!


"Lazima kuna kitu atakuwa amepanga dhidi yako!"


Afande Andrea akaongea kwa wasiwasi!


"Na ndo maana nikawaita mnisaidie...


Butu aliongea kwa sauti ya unyonge,akaweka tuo,lengo awape muda hata wa sekunde kadhaa watu wale wayatafakari maneno yake,kisha akaweka kazi yake mezani


...uzuri zaidi jioni sote tutakuwa nyumbani basi kabla ya saa tatu i mean kwanzia saa mbili na nusu muwepo kivulini pale na nguo zenu za kiraia mimi nitafika hiyo saa tatu nitachelewa kidogo kusudi mtu huyo awai kufika kabla yangu then tutamtia nguvuni sawa?!"


Maaskari wale wakakubaliana!


Saa mbili mbili na nusu maaskari wale wa tatu akiwepo inspekta Jonathan rafiki yake mkubwa na inspekta Butu,afande Paul,pamoja na Andrea waliwasili katika bar ile...


Ilikuwa ni bar tulivu,gari kadhaa ziliegeshwa katika eneo maalumu yalikuwa ni mandhari yalopendeza na kuvutia usoni mwa yeyote awewapo eneo lile...


Jona na Andrea wakatafuta siti na kuketi!


"Mambo mrembo,naweza kukupa kampani?!"


"mh karibu!"


Paul kusudi asishtukiwe akaomba aketi na binti alokuwa peke yake,kila mmoja akaagiza kinywaji stori zikaendelea!


Punde nje iliwasili gari ya kifahari aina ya Bmw lx 224 akashuka kijana mmoja alovaa suti ilo mkaa vyema akafungua mlango kisha akashuka mtu umri wa makamo,mtu huyu nyuma aliongozana

na walinzi wake wawili,wote walivaa suti nyeusi,taratibu akaanza kuufata mlango wa bar ile kabla ajaufikia meseji ikaingia katika simu ya mmoja wa walinzi wake!


"Mkuu huku ndani kuna nyigu watatu!"


Mtu yule alotumiwa meseji akamweleza bosi wake aliyeachia kicheko!


"Najua!,ila sina budi kuingia"


Mtu yule akaingia,akatafuta sehemu nzuri akaketi!


Sasa akawa akiangaza macho eneo lile la bar macho yake yalipogongana na ya yule bint aloketi na Paul wote wakatabasamu!.


Inspekta Butu aliwasili nje ya bar ile,akapaki gari yake pembeni ya Bmw ambayo akuitilia shaka kabisa,akutaka kushuka,pasina kupewa maelekezo!,akasubiri...


"Kuna mtu kaingia,ana walinzi wawili,ni mtu wa makamo"


Kabla ajaijibu ghafla simu yake ikaita


"MR X" ndiyo jina alilolisoma akapokea...


"Nishawasili karibu ndani nimekaa uku katika viti vya mwisho mwisho kabisa"


Butu akashuka katika gari yake aka angalia angalia nje ya bar ile ila hakuna alichotilia shaka akazama ndani!


Baada ya mtu yule kuketi aliongea kitu na wale walinzi wake wakatoka,bado maaskari walifatilia kila kitu.


Butu akaingia na kuelekea mpaka eneo aliloelekezwa,wakati Butu akifika pale wale walinzi walishafika nje wakaingia ndani ya Bmw na kuondoka!,


Butu alimfikia mtu wake,huku akitabasamu akamuuliza....


...Sijui ni wewe tulikuwa tukiwasiliana?!"


"Ndiyo ni mimi!,karibu uketi tuzungumze nasikia wanitafuta sana"


Kauli ile ilimdhibitishia kwamba mtu yule ndiye pale pale tabasamu lake lile la bandia likatoweka fumba na kufumbua akachomoa bastola na kumuelekezea yule mzee!,akamweka chini ya ulinzi,na hata maaskar wale wa tatu wakachomoa bastola zao na kumuelekezea mzee yule,


Mzee alibaki kutoa tabasamu!


Watu walibaki kushangaa tukio lile,


"Taratibu usijiguse naomba tutoke hapa si sehemu nzuri ya kupigia story twende eneo zuri,ulijua sitakukamata siyo?!"


Butu aliongea kwa kiburi mzee wala akuzungumza kitu wakamtoa mpaka ndani ya gari alokuja nayo Butu


Wakamwingiza


Mbele katika usukani aliketi Butu,pembeni yake akaketi Inspekta Jonathani,siti ya nyuma aliketi pembeni Paul mkononi akiwa na bastola ndogo katikati aliketi mzee yule wa makamo na pembeni yake akaketi afande Andrea naye silaha yake akiwa kamnyo oshea mzee yule!


'Hatimaye nimempata,ntamuua kifo kibaya sana ntamchuna ngozi akiwa hai mpumbavu sana huyu'


Butu akawaza,akawasha gari lengo ni kuelekea msitu tasa,palepale alipoipotezea familia yake,palepale alipo muulia Zuberi,usiku huu akapanga kwenda kumfyekelea mzee huyu!,amalize kazi yake,awe huru!





Inspekta wa jeshi la polisi John Butu bado yupo katika harakati zake za kulipiza kisasi,


Anafanikiwa kumtia nguvuni mtu aliyekuwa akihisi kuwa ndiye muuaji wa familia yake,ni baada ya mtu huyo kuhitaji kuonana naye,akisaidiana na maaskari wenzake wanamuingiza ndani ya gari na safari ya kuelekea msitu tasa inafatia,lengo ni kwenda kumuulia huko,je watafanikiwa na nini kitaendelea?!


tusonge katika:


HATUA YA KUMI:


Ulikuwa ni mwendo wa dakika 45 kutoka pale kivulini bar mpaka katikati ya pori tasa,


Hatimaye wakamshusha mzee yule chini,wakaanza kumpiga kwa kumchangia pasina huruma,mwili wote uliharibiwa uso ulichakazwa,mpaka wanamuua walishamtesa sana,saa tisa za usiku ndipo walipo maliza shughuli zote wakaingia ndani ya gari yao tayari kurejea nyumbani,mwili ule wakiwaachia wanyama wa mwituni!


Butu baada ya kufika nyumbani kwake kitu cha kwanza aliweka simu ya yule marehemu chaji,lengo aikague,kisha akaweka na yake alafu akaelekea bafuni kuoga,alipotoka akaelekea kwenye simu yake,kwa kuwa alisikia mlio wa meseji akiwa bafuni,akaifungua hiyo sms na kuanza kuisoma,kila neno alilosoma lilimfanya atoe jicho la mshangao!


Malipo ya msaliti kwetu ni kifo,baada ya kugundua huyu ndo msaliti wetu akunyetishaye siri zetu tumeamua kumuhukumu kwa kukutumia wewe mwenyewe,well done mkuu kaz njema...


Kucheki namba ni zile zile 0759427653


Ina maana yule walo mwangamiza ndani ya dk 45 nyuma siyo 'Mr x?!' ni nani sasa?!,


Palepale akazikumbuka namba '15551' mmiliki wa namba hizi ndiye alikuwa mnyetishaji wake pekee,ndiye aliyempa siri ya madawa yale ya kulevya,na hata walipowakamata pia akampa siri kuwa wanafukuziwa nyuma na mbele kuna tipa la mchanga,baada ya hapo akupata kuiona tena sms yake,ina maana ndo huyu amekuja kumuua tena kikatili namna ile?!,hapana mtu yule akustahili kufa,kwa nini lakini akubali kubeba jukumu lile la kujifanya 'Mr x'?,haraka Butu akaifata simu ya marehemu na kuiwasha,kwani iliisha chaji kabisa,ilipowaka tu ikasoma 'secrety line' ikiwa ndo jina la mtandao, alipokagua upande wa namba zilizokwepo katika simu ile alikuta namba yake tu!,kwa mantiki hiyo line ile ilikuwa ni kwa ajili yake tu au,hapana akakataa bila shaka namba nyingine zilifutwa,haraka akajipigia kuhakikisha namba zile ni kweli zilikuwa ni zilezile '15551' sasa Butu alielekea kuchanganyikiwa kuna siri kubwa sana ilijificha hapo kati na ilikuwa lazima aitambue,kwanza ilikuwa lazima amjue mtu yule familia yake,kazi alokuwa akifanya na hata marafiki zake,palepale akapata wazo,saa kumi ile ile akaingia ndani ya gari lake tayari kurudi kule msituni lengo akauchukue ule mwili autangaze ndugu zake wapatikane,upelelezi wake ndo auanzie hapo!...


Kwa kuwa njiani hapakuwa na magari alfajiri ile alifika katika msitu ule ila alishtuka kutoukuta ule mwili!,akutaka kujidanganya kwamba utakuwa ushaliwa na wanyama mpaka kumalizika lazima kungekuwa na mabaki ya nyama,mifupa ila hapakuwa na kitu kama icho,hata alipotazama vizuri chini akuona mburuzo ambao ungemfanya aamini kuwa mtu yule kabebwa na wanyama,hali ile ikazidi kumchanganya,akarejea ndani ya gari lake na kuliondoa taratibu,alielekea moja kwa moja kazini kwani kulishapambazuka kabisa.


Usiku ule akulala kabisa.


Alipofika kitu cha kwanza aliwaita rafiki zake wale wa tatu na kuwaelezea kila kitu alichogundua,wote walichoka...


"Afande ningeona uachane na wazo la kulipiza kisasi,muachie Mungu pekee aifanye kazi yake tutaendelea kuua viumbe visivyo na hatia mpaka lini?!"


Inspeka Jona akamshauri rafiki yake,


Butu hakuwa tayari kwa hilo,alishakula kiapo mbele ya makaburi ya familia yake kumuua yule alosababisha kuipoteza familia yake kivipi amuache mtu huyo aendelee kudunda?!


"Jona mbona unakuwa wa kwanza kukata tamaa na kunshauri nimwachie Mungu awahukumu,jua fika hapa pia mimi nakusaidia..."


"Ishia hapo hapo Inspekta,tena unyamaze kabisa usiseme kitu,we unanisaidia au unafanya kazi kwangu iendelee kuwa ngumu kila unapo ua upati hata muda wa kufikiria yule wa kwanza mwandishi namba zake ziliakiwa uka ua,huyu naye umeua,je tungemfikisha kwenye vyombo vya sheria?,si ndo ungekuwa mwanzo mzuri wa kumjua adui wa familia yako..."


Jona akaja juu tena akiongea kwa hasira,


"Andrea mbona unaonekana una mawazo sana?!"


Butu Wala hata akuangaika kumjibu Jona akampachika swali askari mmoja aliyeonekana kweli na mawazo!,


"Mi nachojaribu kuwaza hapa na kujiuliza,kama mtu yule alikuwa upande wako kwa nini alikubali kujitoa sadaka? tulimtesa sana,tukampigasi angetuonesha ishara yeyote kwa nini akubali kufa kama 'Mr x'?"


"ilo nalo neno!"


afande Paul naye akadakia


"Na ndo maana nikawashirikisha nyinyi makusudi kwa kugundua mwenyewe sitoweza kuucheza huu mchezo bila msaada wenu...."


Ghafla mlango ukagongwa na askar mmoja akaingia wote wakakaa kimya kumsikiliza...


"Afande Butu unaitwa juu kwa mkuu!"


Wote wa nne wakashtuka,askari yule mleta taharifa akaondoka zake!


"Tukaendelee na kazi,mi ngoja nikamsikilize mkuu"


Wote wakatoka,Butu akaelekea upande zilipo ofisi ya kamishna akaingia,alimkuta mkuu wake akiwa bize na ma faili,alipo muona akaacha lile zoezi alilokuwa akifanya,akafungua droo lake na kutoa bahasha akamkabidhi!


"Hii ya nini tena mkuu?!"


"Barua ipo mkononi mwako soma kilichomo ndani utajua"


Kamishna Nurdin aliongea kimkato macho yake akayarudisha chini,kwenye makalabrasha yaliyopo mezani!


'Nafanya hivi kukusaidia yapaswa ukakae nje kidogo ya jiji hili ukae sawa,'


Nurdin aliwaza wakati huo macho yake yalikuwa katika mafaili,hakuweza kuona mabadiliko alokuwa nayo usoni,Butu alikunja mdomo mishipa ya kichwa ikatuna,


"Mkuu kuliko kuama huu mkoa afadhali niache kazi,sipo tayari kwa huu uamisho.."


"lakini kumbuka uamisho huu umetoka kwa IGP"


"Aijalishi ila sito ondoka ndani ya jiji hili mtanisamehe mkuu"


Palepale Butu akatoka na kuelekea ofisini kwake alipoandika barua ya kuomba kuacha kazi!....


Baada ya kuikamilisha akarejea nayo ofisini kwa mkuu wake na kumkabidhi...


ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

BLOG