Search This Blog

Wednesday, November 18, 2020

X SEHEMU YA 5/10

   


X  

WRITER…………………………………………EDDAZARIA G.MSULWA


WEBSITE………………………………………… www.storyzaeddytz.com
CONTACT……………………………………….. 0657072588/0768516188
AGE……………..18+

SEHEMU YA 5 KATI YA 10


Nilizungumza huku nikishika nikimrudishia Willy simu yake.

“Hicho ni kipengele kifupi walicho kiachia katika website yao dakika tano zilizo pita”

“Ina maana wao ndio wamehusika?”

“Pajero aliuliza?”

“Ndio, ila ina semekana kuna maraisi kama ishirini na mbili hivi walisha ondoka ukumbini akiwemo waziri mkuu wenu”

“Oooh asante Mungu”

Pajero alishukuru kwani kiongozi wao mkuu ameepuka kifo hicho.

“Ina bidi turudi Japani leo hii hii?”

“Nashukuru natamani sana kukutana na ndugu zangu ila nina shindwa kutokana na haya mamlaka niliyo nayo au ikiwezekana wapite hapa waniage wakiwa wana elekea Japani”

“Sawa tutapita ngoja tukajiandae”

Pajero akaondoka eneo hili. Nikaelekea kwenye chumba walipo washauri wa raisi.

“Poleni sana”

“Tuna shukuru sana. Vipi hali ya muheshimiwa raisi kwa maana kuna mpango mbaya tumeusikia juu ya taifa letu?”

“Muheshimiwa amefariki duninia”

“Ohoo MUNGU wangu!!”

Wazee walihamaki sana huku wakionekana kujawa na simanzi kubwa sana.

“Sumu aliyo ivuta iliharibu sanaa mfumo wa mwiliwake kuanzia kichwani hadi moyoni. Hivyo imepelekea muheshimiwa raisi kupoteza maisha yake”

“Ehee huu ni msiba wa taifa jamani”

“Kitu kingine waziri mkuu naye amajiudhuru katikati ya sherehe za uhuru”

“Kwa nini?”

“Hakuna anaye jua hiyo sababu. Hivyo nimeapiswa kuwa raisi wa muda hadi pale uchaguzi mwengine utakapo fanyika. Najua tupo kwenye maombolezo ila hakuna jinsi zaidi ya kurudi nchini Tanzania na mwili wa mpendwa wetu”

“Ni kweli bora turudi Tanzania. Kama uta hitaji ushauri wetu kwenye kuingoza nchi tuta kuwa nawe bega kwa bega. Pia tuna shukuru kwa kutuma watu kutuokoa kwa manaa maisha yetu tulisha jua kwamba yanaisha”

“Musijali ni jukumu langu kuhakikisha kwamba kila mmoja ana kuwa salama. Kama walituzidi akili kwenye kumlinda raisi basi isiwe hadi kwenu”

“Tuna shukuru sana.”

“Ukumbi wa mkutano ulipo kuwa una fanyika, Al-quida wana vamia na habari iliyopo hivi sasa ni kwamba. Karibia viongozi ishirini na kitu hivi waliondoka ukumbini pale kabla ya mlipuko na walio salia basi hatuna uhakika kama wapo hai au laa”

“Mmm sasa inakuwaje muheshimiwa raisi?”

“Tuna rudi nyumbani na mwili wa muheshimiwa wetu”

“Hapo sawa kwa maana nina ogopa sana kuendelea kuwa hapa”

“Mumeniambia kwamba kuna habari mbaya juu ya taifa mumeishikia niambeni?”

“Mmoja wa watekaji alikuwa ana tulazimisha kutoa siri za nchi ila hatukuweza kutoa ila wakatuambia kwamba nchi ina kwenda kutetezwa kama sodoma na gomora hivyo hatutajua ni kipi kina kwenda kuteketeza nchi”

Judy akaingia ndani hapa huku akiwa na simu mkononi mwake.

“Mkuu waziri aliye jiudhuru ana hitaji kuzungumza na wewe?”

Nikaichukua simu hii na nikaiweka sikioni mwangu”

“Ndio”

“Samahani sana Eddy nimeshindwa kuwakilisha vyema kile nilicho paswa kuwakilisha”

“Tatizo lilikuwa ni nini?”

“Mkuu niliweza kupigiwa simu na waziri mkuu aliye jiondoa madarakani. Lisaa moja kabla si kufika uwanjani. Akanieleza kwamba ina ni lazima nihakikishe kwamba nina jiuluzulu la sivyo ame activate silaza zote za nyuklia na zina kwenda kulipua nchi nzima. Nikaona ni vyema kuachia madaraka kuliko kuona nchi ina kwenda kuwa ziwa la moto”

Nikashusha pumzi nyingi sana huku nikiwatazama wazee hawa.

“Code za silaha za nyuklia si anazifahamu raisi yeye peke yake?”

“Raisi alisha zitoa kwa makamu wake miezi kadhaa nyuma hilo jambo nina lijua mimi, raisi na makamu wake”

“Shit kwa hiyo yeye ndio alijisajili kwenye code hizo?”

“Ndio, Samahani sana Eddy”

“Umefanya maamuzi sahihi, wewe ni shujaa na nafasi yako ipo na hakikisha kwamba una jiandaa kusimama kuwa raisi ajeye baada ya kumaliza kipindi changu hichi. Una nielewa”

“Ndio Eddy”

Nikakata simu huku nikiwatazama washauri hawa wa raisi.

“Active code za silaha za nyuklia anazo nani?”

“Ni raisi aliye fariki tu ndio anazo”

Mzee mmoja alinijubu.

“Maria bado hajafika?”

“Wamaeshafika hapa uwanjani na ndani ya dakika tano wana ingia kwenye ndege kwa shuhuli kidogo zime yumba hapo uwanjani. Wananchi wa mataifa mbalimbali nao wana hitaji kuondoka nchini hapa na kurudi makwao kutokana na hili lililo tokea”

“Hakikisha ana pita kwa haraka na ana ingia hapa akiwa salama”

“Sawa”

“Wazee wangu nina kuja”

Nikatoka ndani hapa na moja kwa moja nikaeleka hadi katika chumba cha marubani.

“Karibu muheshimiwa raisi.”

“Nashukuru, mupo tayari kwa safari?”

“Ndio mkuu”

“Nina imani mumepokea taarifa kwamba tuna ondoka”

“Ndio ndio”

“Nashukuru”

Nikarudi katika chumba cha watu wa I.T nikamkuta Willy akiwa bize na wafanyakazi hao wakiendelea kucheza na computer zao.

“Willy nina kuomba”

Willy akasimama na tukatoka nje.

“Nchi ipo kwenye hali ya hatari. Silaha za nyuklia tunazo zitengeneza zina ongozwa kwa code maalumu. Sasa hiyo code anayo makamu wa raisi ambaye una jua timbwili lake”

“Ndio kaka”

“Nina hitaji uweze kufanya kila liwezekanalo kuhakikisha code ina badilika juu kwa juu”

“Sasa mfumo huo wa kuingia katika hizo silaha ni upi siufahamu”

Kwa pamoja tukarudi katika chumba hichi cha watu wa I.T. Kabla hata sijazungumza chochote, tv moja ikaonyesha ramani ya Tanzania, kisha alama nyekundu nyekundu zikaanza kuonekana kwenye mikoa ya kuanzia kusini huku alama hizo zikisambaa kwa kasi sana nchi nzima.

“Ohoo Mungu wangu!!”

Nilizungumza huku macho yakinitoka kwani alama hizi zina ashiria kwamba code inayo tumika kuwasha mabomu ya nyuklia zimesha tumika na kuna lisaa moja kabla ya mabomu hayo kulipuka na yakilipuka nchi nzima ina kwenda kuteketea na kuwa kisiwa cha moto. Simu yangu ikaanza kuita, nikaitoa mfukoni na kukuta ni nambaya makamu wa raisi.

“Muda wa wewe kujiudhuru ume fika. Mimi ndio raisi na nina shikilia kitu muhimu kama nchi. Una lisaa moja kujitangaza una jiudhuru la sivyo, mke wako, wakwe zako. Yatima wezako na watanzania wengine wote wana kwenda kuteketea leo hii. Maamuzi ni yako, cheo au familia”

Baada ya maneno hayo makamu wa raisi akakata simu na nikajikuta mapigo yangu ya moyo yakianza kunienda kasi huku jasho likianza kunichuruzika usoni mwangu kwani katika kitu ambacho makamu wa raisi amejua kunikamata basi ni hapa sina ujanja.


“Muheshimiwa raisi nyukli system ipo active tuna fanyaje?”

Mkuu wa kitengo hichi cha I.T ikulu alizungumza huku akinitazama usoni mwangu. Nikavuta pumzi nyingi huku nikisikilizia jinsi mapigo yangu ya moyo yanavyo kwenda kwa kasi. Judy akaingia kwa kasi ndani hapa na kunikabidhi simu ambayo tayari imesha pokelewa.

“Muheshimiwa raisi ni mimi madame Caro. Tunaona nyuklia system imewekwa ON, ni nini kinacho endelea?”

Madame Caro mkuu wa kitengo cha NSS, aliniuliza huku akionekana kuwa na wasiwasi.

“Sifahamu ni nani ambaye ame activate hizo silaha.”

“Ila code hizo huwa nazo raisi pekee ime kuwaje amezi activate ikiwa raisi amesha fariki dunini?”

“Kwani hakuna njia na namna ya kulizuia hilo jambo?”

“Kusema kweli haiwezekani muheshimiwa raisi”

“Tuna wasilana kwa video call baada ya dakika moja.”

“Sawa muheshimiwa”

Nikamrudishia simu Judy.

“Willy na wewe nina wahitaji ofisini”

“Sawa”

“Judy niitie wazee. Maria amefika?”

“Ndio amesha fika”

“Muambie aje naye”

“Sawa muheshimiwa”

Nikaelekea moja kwa moja katika ofisi ya raisi iliyomo ndani ya ndege hii kwani eneo hili ndio la kuongozea shuhuli zote za kiserikali, pale raisi anapo kuwa ndani ya ndege. Maria akaingia ndani hapa huku macho yakiwa yamemvimba kutokana na kulia.

“Maria nina tambua kwamba tumepoteza mtu muhimu sana ndani ya nchi ila kwa sasa ina bidi tuweke akili zetu kwenye hili lililopo mbele yetu. Kuna shambulizi la silaha za nyuklia linalo kwenda kutokea ndani ya nchi ya Tanzania. Mabomu ya nyuklia yote yapo active na hivi na yana kwenda kushumbulia Tanzania nzima hivyo ndani ya dakika arobaini na tisa zijazo nchi ita kuwa katika hatari ya kulipuka”

“Mungu wangu, hizo code si anazo raisi peke yake?”

“Ndio hivyo, ila ukweli ni kwamba makamu wa raisi naye anazo na yeye ndio amezi activate na amenishinikiza kwamba niweze kujitangaza kwamba nina jivua nafasi ya uongozi na nchi ita baki bila ya kuwa na raisi”

“Hivi huyu mzee ana shida gani. Anashindwa kufanya vitu vingine hadi ana kazania madaraka, yata mpeleka wapi?”

Maria alilalama huku akinitazama usoni mwangu.

“Kama una jua hizi code tafadhali niambie”

Maria akaka kimya kwa dakika kama mbili, washauri wa raisi wakaingia ofisini hapa, wakaingia na Willy na mkuu wa kitengo cha I.T katika ndege ya raisi kwani mfumo wa mzima wa uendeshaji wa ndege hii ume tawaliwa na teknolojia. Tv kubwa iliyopo ofisiini hapa ikawashwa na tukaunganishwa moja kwa moja na ikulu, kitengo cha NSS, kitengo kinacho husika na maswala ya kutengeneza silaha hizo za nyuklia ambacho kipo chini ya jeshi. Nikazitazama dakika arobaini na mbili kati ya lisaa nilizo pewa jinsi zinavyo katika taratibu na pia ndio dakika ambazo mabomu hayo yana kwenda kulipuka.

“Muheshimiwa raisi nini tuna fanya?”

Mkuu wa kitengo cha NSS aliniuliza huku nikitazamana naye kupitia mawasiliano haya ya moja kwa moja ya tv.

“Nime kumbuka”

Maria alizungumza na kwa haraka akanyanyuka kwenye kiti alicho kalia, akazunguka kwenye meza yangu na akawasha computer hii ya raisi. Akaingiza namba za siri kwa mana yeye ni sekretari wa raisi ni mambo mengi sana ana yafahamu ndani ya ofisi ya raisi kupita sisi sote. Akaendelea kuminya minya batani za computer hii.

“Una tafuta nini?”

Nilimnong’oneza Maria aliye inama pembeni yangu.

“Natafuta code kuna faili moja la siri la raisi kwenye mtandoa wa raisi huwa ana lificha na mimi pekee ndio ninaye fahamu hivyo ndio nina angalia kama nita liona”

“Sawa”

Maria aliendelea kutafuta katika computer hii.

‘Dakika arobaini’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikizitazama dakika hizo pembeni ya saa ndogo niliyo iweka hapa mezani.

“Nimezipata. Muna weza kuzinakili”

Maria aliwaambia watu walipo ikulu kwani ndio kuna mfumo mzima wa kuendeshea mabomu hayo ya nyuklia.

“Ndio una weza kuzitaja”

“Kwa herufi kubwa KLKH889W1268076A6UP6666TZ”

Maria alizitaja kwa uharaka mkubwa na zikanakiliwa na kuingizwa na mtu aliyopo ikuku kwenye comnading room. Macho yakatutoka sote mara baada ya kuona maandishi yanayo sema namba hizo sio sahihi na zimabadilishwa miezi miwili iliyo pita.

“Ila raisi hakuniambia kwamba ame badilisha hizi code na sio kawaida yake”

Maria alizungumza huku akiwa na wasiwasi mkubwa sana.

“Kwa hiyo imeshindikana?”

Nilimuuliza kijana wa Ikulu huku wakiongozwa na chief secretary ambaye nilimchimba biti juu ya kumpeleka mwanaye nchini Somalia kwenye vita.

“Ndio muheshimiwa raisi”

“Ina bidi tumtafute makamu wa raisi mstafu aweze kutusaidia katika hili”

Mwana mama huyu ambaye ndio chief secretary wa ofisi hii ya raisi alizungumza huku akitutazama.

“Ndio makamu wa raisi ana weza kufahamu mkuu”

Luteni jenerali alishauri.

“Makamu wa raisi mstafu hapaswi kuingia kwenye hili. Willy fanya unacho weza kufanya nakuamini mdogo wangu. Wewe ndio shabaha yangu ya mwisho. Tafadhali usiniangushe”

Nilimuambia Willy huku nikimtazama usoni mwake.

“Sawa kaka”

“Mpeni Willy ushirikiano wa kila kitu”

“Sawa muheshimiwa raisi”

Mkuu wa I.T alizungumza kisha wakatoka ndani hapa na kuelekea katik chumba chao. Judy akaingia ofisini hapa na moja kwa moja akanifwata na kuni nong’oneza sikioni mwangu.

“Mkuu wale Wajapani wamefika wapo hapo nje ya ndege”

“Waruhusuni kuingia”

“Ila mkuu kumbuka wale sio raisi wa Tanzania hawapaswi kuingia ndani ya hii ndege, na ni kinyume na taratibu za kisheria”

Judy alizungumza huku akininong’oneza sikioni mwangu. Nikamtazama machoni mwake kwa dakika kadhaa.

“Waambie waingie bwana, kuna wakati sheria ina bidi kuvunjwa ili mambo mengine yafanyike. Wana ingia kwa amri yangu”

“Sawa mkuu”

Judy alikubali kishongo upande kisha akatoka ndani hapa.

“Nina kuja nipeni dakika tano”

Nikanyanyuka na nikatoka ndani hapa hapa, nikakutana na rafiki zangu ambao wamenisaidia kwenye mambo mengi. Nikaingia nao kwenye ofisi nyingine ya mkutano kwa ajili ya mazungumzi.

“Aisee muna ndege kubwa sana”

“Nina washukuru sana ndugu zangu kwa kila jambo mulilo nisaidie kusema kweli mume kuwa ni watu wema na wenye kujitao sana sina cha kuwaliwapa”

“Wewe ni ndugu yetu na kama unavyo jua mila na desturi zetu za Kininja”

“Ila Eddy una onekana haupo sawa.”

“Ndugu zangu nimechanganyikiwa kama munavyo fahamu nime kabidhiwa madaraka makubwa kipindi ambacho sijui A wala Z. Hapa ninapo zungumza mabomu ya nyuklia tunayo yatengeneza nchini kwetu yapo yamewashwa na makamu wa raisi aliye kuwa amewateka hawa watu. Hivyo kuna kama nusu saa kabla ya kulipuka na au nitangaze kujiudhuru uraisi. Najua hizi ni siri kubwa za kiseerikali ila sina namna zaidi ya kuwaambia”

“Tuna elewa ndugu yetu. Akira ume bobwea kwenye haya mambo una weza kuwasidia”

“Akira ndugu yangu kama una fahamu nina omba msaada wako”

“Code ya zamani ipo?”

“Ndio”

“Sawa tuna weza kufanya backup”

Akira alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.

“Njoo”

Nikatoka na Akira ndani hapa na moja kwa moja nikaingia naaye kwenye chumba cha I.T.

“Willy wapi umefikia?”

“Kaka kusema kweli nina changanyikiwa hivi vitu sina utaalamu nao kabisa”

“Hembu mpisheni huyu jamaa”

Akira akachagua moja ya computer atakayo fanyika kazi. Akazikunja nywele zake ndefu na kuziweka kama kichuguu na akazibana na moja ya pini ambayo ina ni silaha kwa sisi maninja tuna zifahamu kwani ukimchana mtu na pina hii, ana kufa ndani ya dakika tatu kwani ina sumu kali sana.

“Code ya zamani ni ipi?”

Akira aliuliza na mkuu wa kitengo hichi cha I.T alizungumza. Akira akaendelea kuifanya kazi hii huku dakika zikizidi kuporomoka.

“Vipi ndugu?”

Nilimuuliza Akira huku zikiwa zimesalia dakika kumi na tano. Akira akninyooshea kidole kimoja akimaanisha dakika moja. Simu yangu ikaanza kuita, nikaitoa mfukoni na kuona namba ya makamu wa raisi, nikavuta pumzi nyingi kisha nikaipokea huku nikipumua taratibu.

“Naona ume amua mke wako na familia yako iweze kufa?”

Akira akaninyooshea dole gumba akimaanisha mambo yana weza kuwa vizuri.

“Sina muda wa kuongea sasa hivi”

Nikakata simu na kuirudisha mfukoni.

‘Dakika kumi’

Nilizungumza kimoyo moyo, huku nikiitazama mikono ya Akira jinsi inavyo zidi kufanya kazi huku katika compter akitumia maandishi ya kijapani ambayo nina jua kuyasoma ila watu wengine hapa ndani akiwemo Willy wana shangaa shangaa na anacho kiandika Akira japo ni kijapani ila mimi mweyewe siwewi kwa maana ni mambo ya code.

‘Daki saba’

Nilizungumza huku mapigo yangu ya moyo yakianza kunidunda kwa kasi kwa maana dakika zina zidi kupungua. Sikutaka kumuuliza chochote Akira kwa maana nina imani ana jua anacho kifanya.

‘Mmmm dakika nne, asije akaibutua nchi yangu huyu?’

Nilianza kujihisi hovyo huku watu wote ndani ya hichi chumba wakiwa na wasiwasi mkubwa na macho yapo kwenye tv ikionyesha jinsi alama hizo nyekundu zilivyo jaa katika ramani yote ya nchi ya Tanzania.

‘Dakika mbili’

Nilizungumza kimoyo moyo huku muda ukiwa umesha kwisha kabisa.

“Tayari”

Akira alizungumza huku akinitazama usoni mwangu. Taratibu tukaanza kuona jinsi alama hizo nyekundu zikianza kufutika kwa kasi kwenye ramani ya nchi ya Tanzania na zote zikatoweka na saa ya bomu hili likasimama sekunde ya thelathini na tisa kabla ya kulipuka. Nikashusha pumzi nyingi sana huku nikimtazama Akira kwa furaha sana.

“Nashukuru sana kaka. Sijui nikupe nini?”

“Mimi na wewe ni ndugu na tumeumbwa kwa kuitetea dunia na watu walimo ndani yake. Ila mfumo huu ina bidi uweze kubadilishwa, ni mfumo wa kizamani sana, ndio maana una weza kuchezewa namna hii”

“Sawa ndugu yangu je una weza kuubadilisha?”

“Ndio na mfumo nilio uweka hapo ni kwa muda tu. Hivyo una weza kubadilika na ukawa salama zaidi”

“Kaka nina kuomba ikiwezekana turudi wote nchini Tanzania, kisha ndio muende japani njoo tuzungumze”

Nilizungumza kwa furaha huku watu wote ndani ya ofisi hii wakishangilia. Nikapita kwenye ofisi yangu na nikasikia shangwe zikitawala kwani ni ushindi. Tukaingia katika ofisi tuliyo tuliyo waacha wengine.

“Vipi mume fanikiwa?”

“Ndio ndugu yangu Akira ameifanya kazi vizuri”

“Huyo ndio mtaalamu tunaye mtegemea kwenye kazi zetu na hata kujua ni eneo gani walipo wazee wako, Yakira ndio aliifanya kazi”

“Sijutii kuwa nanyi kwenye maisha yangu. Ndugu zangu nina waomba ombi la mwisho. Nina waomba turudi nchini Tanzania, ndugu yangu akarekebishe mifumo yetu ya kitekenolojia na kuwafundisha ndugu zangu. Hata kuwalipa nipo tayari kwenye hili”

“Usijali wewe ni ndugu yetu. Tuta kuunga mkono kwenye kila utakacho tuomba”

“Nina washukuru sana basi nita mleta mkuu wa kitengo cha usalama wa raisi ili niwatambulishe asije akaona mapicha picha kuwaona ndani ya ndege hii”

“Sawa sawa”

Nikatoka ofisini hapa na nikaingia katika ofisi ya raisi wazee wote wakaanza kunipongeza na Maria akanikumbatia kwa furaha, japo tupo kwenye msiba wa raisi ila ni heri msiba wa mtu mmoja kulilo kuizika Tanzania nzima kwani tuta kuwa tume ifuta kwenye ramani ya dunia.

Nikamuita mlinzi namba moja wa raisi na nika mtambulishwa kwa marafiki zangu hawa na nikaweleza kwamba wao ndio walio tuokoa kwenye hili. Tukawatambulisha kwa baadhi ya walinzi wa ndege hii ya raisi.

“Mkuu”

Judy aliniita, nikatoka ndani ya ofisi hii.

“Niambie”

“Nimezungumza na Gody ameniambia kwamba mwili wa raisi upo tayari umeandaliwa kwa ajili ya kuletwa huku”

“Umesha wekwa ndani ya jeneza?”

“Ndio”

“Basi waulete ili tuweze kuondoka nao kwa maana hatuna muda wa kuendelea kukaa hapa nchi yenye imesha ingia kwenye matatizo”

“Sawa mkuu”

Judy akaondoka eneo hili. Willy akanifwata huku akiwa amejawa na tabasamu pana sana usoni mwake.

“Aisee kaka huyo jamaa ni kichwa sana. Ina bidi uniiunganishe naye nipate maujuzi kwa maana ile kasi ya kuunda code aliyo kuwa nayo kwa kweli mimi simfikii hata robo?”

“Usijali tuna kwenda nao Tanzania na jitahidi ukae nao karibu wakufundishe haya mambo”

“Aise kaka ni jambo zuri sana. Ehee ina kuwaje kwa huyu mshenzi kwa maana mtu anapo amua kulipua nchi kwa ajili ya matakwa yake mwenyewe sio jambo la kawaida”

“Ngoja nirudi nyumbani nikakae pale mjengoni alafu yule mshenzi ndio ata nijua alilea na kukuza kichaa. Kwanza mali zake zote za Tanzania tuna zipiga chini, akaunti zake zote tuna zifunga alafu tuone hiyo Scropion ita fanya nini?”

“Ila ingekuwa vizuri kuwazuia hao Scrorpion moja kwa moja kuliko yeye kaka kwa maana yeye ndio kiongozi wao na katika huu mlipuko ulio tokea nin aimani kwamba wao wame wawezesha Al-quida kufanya mlipuko huo kwa maana Al-quida sidhani kwamba wana uwezo wa kuifanya hii kazi bila msaada”

“Sasa nina anza kupata picha?”

“Picha gani?”

“Una kumbuka kile kipindi nilikuambia makamu wa raisi ameniita kwake na kunipa kazi ya kuwaua baadhi ya maraisi kwenye huu mkutano utakapo kuwa una fanyika nili mkatalia?”

“Ndio kaka nina kumbuka”

“Hembu nipe listi ya maraisi walio toka kabla ya mlipuko”

Willy akatoa simu yake mfukoni na kunionyesha majina ya maraisi walio wahi kutoka kabla ya mlipuko. Maraisi kumi na tano kati ya ishirini na mbili walio toka wapo kwenye kundi la Scorpion na wanaendeshwa na makamu wa raisi na saba walio salia ni maraisi wanao pinga umoja huo na wengine walio salia ndani ya ukumbi wengi wao ni maraisi walio tamani kujitoa kwenye umoja huo wakashindwa.

“Huyu mshenzi siku nikimshika nina mnyonya damu, haki ya Mungu”

“Kaka una onaje tukazitoa siri zake hadharani kwania kiendelea hivi ata tuona sisi ni viji midoli vyake”

“Ngoja tufike Tanzania”

“Sawa kaka”

Jeneza lenye mwili wa raisi likafikishwa uwanjani hapa, kutokana na taratibu za kijeshi tukaupokea kwa heshima kubwa huku jeneza lake likiwa limefunikwa kwa bendera ya Tanzania. Jeneza lake lika weka eneo la mizogo ya ndege hii. Tukaukagua kwa mara nyingine kudbihitisha kwamba ni mwili wake na tukaridhika kwamba ni mwili wa raisi wetu.

“Muheshimiwa raisi ni wakati wa kulihutubia taifa na kuwaleza juu ya msiba huu mzito wa raisi wetu”

Mshauri mkuu wa raisi alizungumza huku akinitazama usoni mwangu, jambo ambalo ni gumu sana kwangu kwani sijui nina anzaje anzaje kuwaambia watanani kwamba raisi wao waliye kuwa wana mpenda na kumpatia kura asilimia themanini kwenye uchaguzi ulio pita kwamba amefariki duniani.



“Ndege ina ondoka baada ya muda gani?”

“Nusu saa mkuu”

Judy alijibu huku akinitazama usoni mwangu.

“Mzee nita toa hutoba hiyo nikiwa angani”

“Hakuan tabu muheshimiwa raisi”

“Judy nifwate ofisini kwangu”

Tukaongozana hadi ofisini, nikaka kwenye kiti changu huku nikiwa na mawazo mengi sana kichwani mwangu.

“Vipi muheshimiwa/”

“Mime beba gunia la misumari ingali kichwani mwangu nina kipara”

“Una maanisha nini?”

“Judy uwezo wangu ni kuongoza jeshi na sio nchi. Hizi siku tisini nina ziona ni siku za mateso sana kwenye maisha yangu, sijui hata nlama nita zimaliza. Kwenye hizi siku tisini sijui nimchague nani awe makamu wa raisin a nani awe waziri mkuu ikiwa watu wenyewe siwaelewi kabisa. Huku kuna wasaliti, huku kuna makamu wa raisi, huku familia yangu ina nihitaji. Yaani nina ona mawenge mawenge. Isitoshe nimekaa kwenye nafasi ikiwa sina kigezo cha umri”

“Nakushauri kama kaka yangu. Umekaa kwenye maisha ya jeshi kwa kipindi kirefu sana, ume ishi maisha ya kushika bunduki na uliweza kuwaongoza rafiki zako kwenye mission nyingi ambazo kwa asilimia tisini na saba zilifanikiwa. Hadi nimefikia umri huu sijawahi kusikia kuna chuo cha kufundisha maraisi, sijawahi na sidhani kama kita wahi kutokea chuo kitakacho fundishi watu waje kuwa maraisi wa nchi zao. Ila najua ipo siasa ambayo ndio hutengeneza hata wale wasio kuwa na elimu kubwa kuja kuwa viongozi wakubwa. Nafasi hii haijakua kwa bahati mbaya ila ume kuja kwa makusudi ya Mungu”

“Dogo acha kumuingiza Mungu kwenye hili. Nina hisi hapa kuna mpango mmoja mbaya ambao una kuja mbele yangu. Sijui ni mpango gani ila nina hisia hizo. Willy aliweza kujawa na hisia za kwamba raisi ana weza asirudi nchini Tanzania na akaniambia na mimi nikamshauri raisi kabla ya kutua tugeuze na turudi Tanzania ila akakataa kato kato, mwisho wa siku nime achiwa msala wa kujibu mbele za wananchi. Inakuwaje”

“Nilizungumza kwa sauti ya unyonge huku nikimtazama Judy machoni mwake. Maria akaingia ofisini hapa na akaka kwenye moja ya kochi.

“Maria bado amezima”

Maria alizugumza kwa sauti iliyo kauka kwa maana amelia sana.

“Maria ndio nani?”

Niliuliza kwa mshangao.

“Ohoo ni la pili la mtoto wa raisi aliye fariki”

“Kumbe ana itwa Maria?”

“Ndio ni wajina wangu, ndio maana baba yake alikuwa ni zaidi ya kiongozi kwangu. Alinilea na kunipenda kama mwanaye wa kumzaa. Aliniambia mambo mengi sana ambayo hata mke wake wa ndoa hayafahamu. Hivyo nime poteza mtu muhimu sana kwenye maisha yangu”

Maria alizungumza kwa sauti ya kusikitisha hadi sisi wenyewe tukamuonea huruma. Tukasikia sauti ikitokea kwenye vipaza, rubani akatujulisha ina tubidi kufunga mikanda ya siti zetu kwani ndege sasa ina anza safari. Nikajifunga mkanda wa siti niliyo ikalia na baada ya dakika tano ndege hii ikaanza kuzunguka taratibu uwanjani hapa ikielekea katika njia ya kurukia. Ukimya ukatawala kati yetu huku sote tukisubiria ndege hii kupaa angani. Baada ya muda mchache ndege ikapaa angani na kutufanya sote tufungue mikanda ya siti zetu. Mshauri mmoja wa raisi akaingia ndani hapa.

“Muheshimiwa raisi ni wakati sasa wa kulihutubia taifa”

“Sawa ila sijui nina kwenda kuzungumza nini?”

“Tayari tumesha kuandalia cha kuzungumza”

“Hembu naomba nipitie”

“Sawa”

Mzee huyu akaniletea karatasi yenye maneno ambayo nina paswa kuzungumza. Nikayasoma na kuyakremisha kisha nikatoka ndani hapa. Nikasimama eneo maalumu ambalo raisi akihitaji kuhutubia huwa ana simama na kwa nyuma kuna nembo ya raisi. Kamera mani akaweka kila kitu tayari kisha nikasimama kwa ajili ya kulihutubia taifia ikiwa ndio mara yangu ya kwanza mara tu baada ya kuapishwa. Kamera mani akanihesabia kwa ishara ya vidole hadi ikatimia tatu na akaniruhusu kuanza kuzungumza.

“Habari Watanzani wezangu. Nina imani wengi wetu muta kuwa muna jiuliza ni kwa nini nimeapishwa na kuwa raisi ikiwa cheo changu ni jenerali wa jeshi. Tukiwa katika ziara yetu nchini Ujerumani, raisi wetu aliweza kushambuliwa kwa hewa ya sumu. Hewa hiyo ya sumu ilifungwa kwenye mfumo wa A/C inayo ingia chumbani kwake na kusababisha sumu hiyo kuleta madara makubwa kwa raisi majira ya usiku alipo kuwa ame lala.”

“Usiku huo huo mara baada ya kugundua utofauti, ika tulazimu kumpeleka muheshimiwa raisi hospitalini kwa ajili ya matibabu ya haraka. Madaktari walifanya kila walicho kiweza ili kuyaokoa maisha ya raisi wetu ila kwa bahati mbaya raisi…….”

Nikakaa kimya huku nikiwatazama watu wanao nifwatilia kwa umakini sana.

“Raisi amefariki duninia majira ya saa tano na dakika ishirini na tano asubuhi kwa saa za huku Ujerumani. Ni masikitiko makubwa na kwa taifa kwa ujumla. Nina tangaza siku za saba za maombolezo ya raisi wetu na zitakuwa ni siku za mapumziko kwa wafanyakazi wa sekta ya serikali na sekta binafsi. Mungu ailaze mabali pema peponi roho ya raisi wetu mpendwa Panteleo.”

Mazungumzo yakaishia hapa nikaondoka eneo hili na moja kwa moja nikaeleka katika chumba changu na nikajifungia kwa ndani na kujikuta machozi yakinimwagika kwa uchungu sana. Mlango ukagongwa.

“Nahitaji kuwa peke yangu”

“Mkuu kuna simu kutoka kwa mke wako”

Judy alizungumza na kunifanya nijifuta machozi kwa kitambaa changu kisha nikafungua mlango na akanikabidhi simu yake ambayo ipo hewani katika mfumo wa video call. Nikakaa kitandani huku nikimtazama Cauther.

“Pole sana mume wangu, najua una pitia kwenye kipindi kizito na upo mwenyewe. Namuomba Mungu akutie nguvu kwenye wakati kama huu, kwani ni wakati ambao rehema za mwenyezi Mungu zina hitajika juu yako”

“Nina shukuru mke wangu. Vipi afya yako ina endeleaje?”

“Afya yangu ipo vizuri kwa ulinzi ulipo hapa nyumbani ilibidi dakatri leo aje hapa hapa nyumbani kuniangalia afya yangu ina kwendaje”

“Mume nina kusikia mimi nipo”

Niliisikia sauti ya Nadia

“Yupo wapi huyo?”

“Huyu hapa”

Cauther akamkabidhi simu mdogo wake.

“Shikamoo shem”

“Marahaba, vipi una endeleaje?”

“Nipo salama. Pole sana kwa matatizo shemeji yangu na pia hongera bwana kwa kuwa raisi”

“Asante, mpe simu Cau”

“Ndio mume wangu”

“Tupo njiani tuna rudi leo hii, hivyo usishangae ukasindikizwa na walinzi hadi ikulu”

“Sawa mume wangu”

“Badae naomba nitulie tulie”

“Sawa mume wangu”

Nikakata simu, nikatoka nje na kumkabidhi Judy simu yake.

“Nina lala kwa masaa mawili nina kuomba uniamshe”

“Sawa mkuu”

Nikarudi kitandani na kujilaza hazikuisha hata dakika kumi Maria akaingia chumbani humu.

“Samahani Eddy kwa kukusumbua”

Maria alizungumza huku akikaa karibu yangu.

“Vipi?”

“Najua tupo kwenye wakati mgumu ila nina omba nitulieza haja za mwili wangu. Nina kuomba sana”

“Maria hivi hata nguvu za kutomb** tuna zitolea wapi rafiki yangu. Hapa nilipo sina stimu kabisa ya kufanya tendo hilo.”

“Eddy naomba nipe niwe sawa tafadhali”

Maria alizngumza huku akinishika shika juu ya zipu yangu na akaanza kumminya minya jogoo wangu itendo kilicho nifanya nimtazame kwa muda na taratibu Maria akaniinamia na akaanza kuninyonya denda. Maria akafungua zipu ya suruali yangu na akamtoa jogoo wangu na kuanza kumnyonya huku akimchua chua. Akanivua suruali kisha ana yeye akavua suruali yake ya kitambaa aliyo vaa pamoja na nguo za ndani kisha akapanda kitandani hapa na akamkalia jogoo wangu taratibu.

“Usipige kelele zako zile”

“Usijali”

Maria akajihudumia yeye mwenyewe hadi akafika kileleni mara tatu mfululizo nami ndio nikamaliza.

“Hapa sasa akili yangu ita fanya kazi vizuri”

Maria alizungumza huku akinilalia kifuani mwangu.

“Kweli?”

“Haki ya Mungu vile una jua mambo mengi yametokea kwa kipindi kimoja hivyo, akili yangu ilivurugika balaa”

Maria akaingia katika bafu lilipo ndani hapa akaoga kisha akavaa nguo zake na akatoka chumbani kwangu.

‘Amenivurugia usingizi wangu’

Nilizungumza huku nikiingia bafuni, nikabadilisha suti niliyo ivaa nami nikatoka hapa.

“Nitafutie Judy muambie anifwate ofisini kwangu”

Nilimuambia mmoja wa walinzi kisha nikaingia ofisini, Judy akaingia.

“Vipi mkuu masaa mawili hayajaisha, niliweka Alarm kabisa ya kukuamsha”

“Usingizi ume katika naona maruwe ruwe. Best nia njaa balaa nipikie basi chakula”

“Una taka kula nini?”

“Kwanza huko jikoni kuna chakula gani?”

“Kipo chakula cha kila aina?”

“Mmmm waambie wanipikie ugali kachumbani na nyama choma”

“Sawa ngoja nikalisimamie hilo”

“Wewe umesha kula?”

“Ndio mimi nilisha kula muda mrefu tu”

“Poa poa, niletee basi soda ya baridi”

“Aina gani?”

“Coca”

“Sawa”

Judy akatoka ndani hapa, nikaanza kukagua kwenye computer hii, viongozi wote walipo serikalini pamoja na sifa zao.

“Asante”

Nilimuambia Judy mara baada ya kuniandalia soda hii.

“Karibu”

“Ehee nime kumbuka jambo kaa hapo”

Judy akaka kwenye kiti.

“Nahitaji uache jeshi”

“Ehee?”

“Ndio nahitaji kukutea kuwa mshauri wangu binafsi tofauti na kazi hiyo ya jeshi kwani wewe ndio mtu unaye nielewa vizuri ukiachana na mke wangu”

“Sawa hakuna shaka, utakapo kuwepo mimi nipo utakapo kufa nami nita kufa hiyo siku kama ni kwenye shambulizi”

“Nashukuru kwa moyo huo Judy. Katika mabinti wa ajabu ambao tumewahi kukutana nao basi wewe ni wa ajabu sana kusema kweli nina kushukuru sana”

“Usijali muheshimiwa, chakula baada ya dakika kama kumi hivi wata kileta”

“Sawa, sasa kazi yako ina anza sasa hivi. Nina miezi mitatu tu ya kuwa kiongozi wa hii nchi. Ni nani ambaye una mendekeza aje kuwa raisi afwataye”

“Wewe”

“Mimi sihitaji hii kazi. Nina ifanya baada ya hapo nina achana nayo ndio maana nilikichagua uwe katika hii nafasi ya kunishauri ili siku nikikabidhi ofisi kwa raisi ajaye basi tuna ondoka watu. Nina jua nikiwaacha kwenye mfumo huu wa serikali na mimi nime acha kazi muta pata tabu sana”

“Sasa muheshimiwa, wewe ume fikiria nani awe raisi ajaye?”

“Kwenye serikali hii ninge pendekeza waziri mkuu agombanie uraisi. Kwanza ni mtu mwenye hekima na ustarabu”

“Ila ana onekana ni mdhaifu kwenyeswlaa kama lile ilikuwa sio rahisi kwa yeye kuajiudhuru hadharani?”

“Alishinikizwa kwa ishu hii ya mabomu ya nyuklia kama alivyo kuwa amefanya makamu wa raisi kwangu, hivyo miezi hii ikiisha basi nita hakikisha ana kuwa kiongozi wa nchi kisha sisi tukampumzike. Wewe na mume wako mutafute nchi ya kwenda kula bata, mimi na mke wangu nikatafute pa kula maisha.”

“Gody naye?”

“Kama ata hitaji kupanda cheo jeshini sawa. Kama ata hitaji kuacha haija shida”

“Uta zungumza naye”

“Yaa nita ogea naye”

Safari ikazidi kusonga mbele huku masaa yakzidi kukatikaka kwa haraka tofauti kabisa na siku ambayo tulianza safari kuelekea nchini Ujerumani. Ndege ikatua katika uwanaja wa mwalimu J. K Nyerera. Taratibu nikafungua kipazia kidogo cha dirishani na nikashuhudia magari mengi ya jeshi na wanajeshi wengi wakiwa uwanjani hapa kwa ajili ya kuupokea mwili wa mpendwa wetu raisi. Wananchi wengi nao wamejitokeza huupokea mwili wa raisi.

“Muheshimiwa ni muda wa wewe kushuka”

Mlinzi mkuu wa raisi alizungumza huku akinitazama usoni mwangu. Nikasimama, nikajiweka sawa mwili wangu kisha taratibu nikatoka ofisini humu. Nikaongozana na walinzi huku wakiwa wamenizunguka kwani majukumu ya uangalizi yamesha badilika na yapo kwangu. Tukaanza kushuka kwenye ndege hii huku waandishi wa bahari wa raisi wakiendelea kurekodi kila jambo. Moja kwa moja nikaelekea hadi katika jukwaa maalumu walilo viongozi mbalimbali wa serikali. Nikasalimiana nao kisha nikaa kwenye kiti ambacho hukalia raisi peke yake akiwa kwenye shuhuli za kiserikali. Taratibu zote za kijeshi zikafanyika na jeneza lenye mwili wa raisi likatolewa ndani ya ndege. Heshima za kijeshi zikafanyika katika mapokezo haya huku vilio vikirindima uwanjani hapa kutoka kwa wana mama walio pokea mwili wa raisi. Utaratibu wa mwili kupelekwa kuhifadhiwa hospitali ya taifa Muhimbili uka fanyika huku mimi na walinzi wangu pamoja na washauri wangu tukielekea ikulu.

Tukafika ikulu na taratibu nikashuka kwenye gari hili maalumu kwa ajili ya raisi.

“Mke wangu amesha fikishwa hapa?”

Nilimuuliza mmoja wa walinzi.

“Ndio muheshimiwa”

“Nahitaji kuonana naye”

Moja kwa moja nikapelekwa hadi katika nyumba ya raisi. Nikamkuta Cauther akiwa na Nadia pamoja na walinzi wa kike. Cauther akanikumbatia kwa furaha huku machozi yakimwagika kwani ni siku ya huzuni.

“Nashukuru Mungu ume rudi salama mume wangu”

“Mungu ni mwema mke wangu”

Nilizungumza huku nikimuachia Cauther, nikamnyonya denda huku nikitazama tumbo lake.

“Kwa hali yako una weza kuambatana na mimi kwenye hizi shuhuli za mazishi?”

“Nita jikaza”

“Shem hali ya dada hapo ilipo sio vizuri akazunguka zunguka. Dada kumbuka dokta alivyo kuambia”

“Sawa”

“Habari wifi”

Judy alimsalimia Cauther.

“Salama shemeji za safari”

“Salama, samahani muheshimi raisi una hitaji commanding room”

Judy alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.

“Sawa Judy nina kuja dakika moja. Mke wangu, wamekuhudumia vizuri?”

“Ndio baby”

“Basi ni jambo la kumshukuru Mungu. Tuta zungumza ngoja nikashuhulikie mambo ya kiserikali.”

“Sawa mume wangu”

Nikambusu Cauther katika lipsi yake kisha nikatoka ndani hapa huku nikiongozana na Judy pamoja na walinzi wengine ambao wana nilinda.

“Kuna nini?”

“Ina bidi ukabidhiwe code zote za siri za kuendesha silaha za nyuklia”

“Sawa sawa”

Tukaingia katika ukumbi huu wa kuongozea oparesheni zote za kiusalama wa nchi.

“Muheshimiwa raisi”

Chief secretary alizungumza huku akinipa mkono.

“Habari yako?”

“Salama”

Nikasalimiana na kila mtu, kisha zoezi la kujisaliji katika mfumo wa kuongoza bomu za nyuklia kwani unahitaji alama za kiganja changu cha mkono wa kulia pamoja na alama za mboni za macho yangu. Baada ya zoezi hili kukamilika, nikarudi nilipo muacha Cauther na mdogo wake. Simu yangu ikaanza kuita, nikaitoa mfukoni na kuona namba ambayo makamu wa raisi ndio anaye ichukua.

“Eddy…..ume kuwa raisi kabla yangu. Hahaaa kweli maisha yana kwenda kasi sanaaaa”

“Una hitaji nini?”

Niliuliza kwa msisitizo mkubwa sana.

“Ninacho hitaji una jua Eddy, ninataka uraisi”

“Ngoja nikuambie jambo moja. Huto kuja kaa uwe raisi kwenye hii nchi. Ukiwa raisi labda mimi niwe nimekufa. Na kitu kingine nikuambie, nina nguvu sasa na nimekuwa raisi wa nchi yenye nguvu kuliko zote duniani. Nita hakikisha nina kusaka na nina kusambaratisha wewe na hilo kundi lako la Scorpion na kifo chako kita kuwa ni cha kinyama sana kwani nita kukata kata kipande kimoja baada ya kingine. Mbwa wewe”

Nilizungumza kwa hasira sana kiasi cha kumfanya mke wangu pamoja na mdogo wake kunishangaa kwani hali niliyo rudi nayo sio niliyo ondoka nayo hapa ndani.



“Vipi mume wangu”

Cauther alinifwata na kusimama mbele yangu. Taratibu akanishika kifuani mwangu huku akisilizia mapigo yanguya moyo jinsi yanavyo kwenda kasi.

“Niambie mume wangu kuna tatizo gani?”

“Kuna mpuuzi ana umiza kichwa changu. Mumesha kabidhiwa vyumba vya kulala?”

“Ndio”

“Twende chumbani kwetu”

Tukaeleka katika chumba chetu cha kulala. Cauther akaanza kunivua koti langu la suti.

“Natamani miezi mitatu ifike hata kesho niachane na hii kazi”

“Usijali mume wangu ita fika tu kwa uwezo wa Mungu”

“Badaye saa moja moja usiku hivi, nikumbushe nizungumze na mzee yule niliye kuja naye nyumbani”

“Sawa mume wangu”

“Kichwa kina niuma sana”

“Nikuletee dawa?”

“No nahitaji kulala kama masaa matatu hivi kisha uta niamsha kwa maana toka nime kwenda sijajua kitanda kipo vipi”

“Sawa baby ina bidi uoge”

“Nitaoga mara baada ya kuamka”

Cauther akanivua viatu pamoja na suruali yangu na nikajilaza huku akili ikiwa na mawazo mengi sana, baada ya muda mfupi usingizi mzito ukanipitia na nikalala fofofo.

“Honey”

Niliisikia sautia ya Cauther ikiniita.

“Saa moja kasoro sasa usiku. Vipi nikuache uendelee kulala?”

“No nimetosheka. Nipatie simu yangu”

Cauther akanipatia simu yangu, nikaitafuta namba ya mzee na nikampigia.

“Shikamoo mzee”

“Marahaba Eddy. Aisee poleni sana”

“Aha tumesha poa mzee wangu. Bwana mzee mambo yamekwenda ndivyo sivyo. Nimekabidhiwa kikombe amabcho sikukihitaji kabisa ina kuwaje hapa?”

“Si kwa muda lakini?”

“Ndio”

“Ukimaliza muda wako achana nayo kabisa hiyo kazi”

“Kwa hiyo ndani ya hii miezi mitatu mimi na watu wangu wa kariu tuta kuwa salama kweli?”

“Ndio muta kuwa salama, hakuna shaka kwenye hilo”

“Sawa nina shukuru mzee wangu nilihiyaji kufahamu hilo tu”

“Sawa sawa, ilikuwaje hadi muheshimiwa akaondoka?”

“Ni mfumo wa A/C yake uliwekewa gesi ya sumu ambayo ilimdhuru sana na hadi tuna mfikisha hospitalini kidogo hali yake ilisha kuwa mbaya. Madaktari walijitahidi ila ika shindikana kabisa kuyaokoa maisha yake”

“Aisee poleni sana”

“Tuna shukuru”

“Mazirishi lini?”

“Bado sijajua kwa maana kiongozi ni mkristo hivyo kuna kamuda kidogo hapa kama ka wiki hivi hadi atakapo zikwa”

“Sawa sawa Eddy nita kuja kumzika ndugu yetu”

“Karibu sana”

“Asantez”

Nikakata simu, nikamkabidhi Cauther aliye kaa pembeni yangu.

“Kweli mume wangu ume choka una zungumza kwa sauti ya upole sana”

“Yaa nime choka sana mke wangu. Nahisi kuchanganyikiwa yaani sijui ni kwa nini mambo yana kwenda kasi kiasi hichi”

“Ni changamoto mume wangu, kila kitu kita kwenda vizuri na tuta achana na maisha haya”

Cauther alizungumza huku kichwa chake akiwa amekilaza kwenye bega langu la upande wa kushoto.

“Sikutegemea siku hata moja nita kuja kuwa raisi hata wa siku moja wa hii nchi”

“Ila kila jambo hutokea kwa mapenzi ya Mungu. Viongozi wakuu watau wa kiserikali wameachia madaraka, haikuwa na jinsi mume wangu kuchukua madaraka hayo.”

“Nahitaji tukimaliza huu muda wa miezi mitatu, nikimkabidhi raisi ajaye ofisi tuna hama nchi kabisa. Sihitaji kabisa kukaa nchini Tanzania”

“Una taka twende wapi?”

“Japani, kuna marafiki zangu jioni ya leo nita kutambulisha tuta pata chakula nao.Ni Wajapani, hivyo nita kwenda kuishi kwenye ile nchi nina imani tuta kuwa mbali sana na nchi za Kiafrika”

“Sawa mume wangu, uendapo mimi nipo nawe, haijalishi tuta ishi maisha gani ila utakapo kwenda nita kufwata hadi kifo kitakapo tutenganisha”

“Nashukuru mke wangu. Ngoja nikaoge”

“Sawa, mimi ngoja nikuandalie supu unywe mwili uchangamke changamke”

“Weka pilipili nyingi”

“Sawa mume wangu”

Nikaingia bafuni nikaoga, nikarudi chumbani na kukuta nguo ambazo Cauther ameniandalia. Nikavaa na kutoka chumbani hapa. Nikamkuta Judy sebleni akizungumza na Cauther pamoja na Nadia.

“Vipi huja kwenda nyumbani kujipumzisha?”

“Hapana mkuu”

“Tukiwa nyumbani niite tu kaka”

“Sawa kaka. Mwili wa raisi umesha hifadhiwa na ulinzi ume imarishwa vizuri sana.”

“Mwanaye na mke wake wapo wapi?”

“Wapo hapa hapa ikulu ila kwenye nyumba kuu ya raisi”

“Okay sasa fanya hivi au ngoja nikaonane nao. Nenda kawachukue hotelini wale Wajapani na uje nao hapa ikulu”

“Sawa sawa”

“Mke wangu twende tukawape pole wafiwa”

“Sawa mume wangu, ngoa nikachukue mtandio kwa maana ina bidi nijistiri”

“Poa, shem vipi wewe huendi?”

“Hapana shemeji mimi nipo nipo hapa kwanza nina sikilizia harufu nzuri ya hapa ikulu. Hivi shem una jua sikuwahi kuingia ikulu toka nizaliwe na leo ndio mara ya kwanza alafu nita lala ikulu, yaani nahisi hadi kuchanganyikiwa”

“Hahaaa vitu vya kawaida hivyo. Uta lala hadi uchoke”

“Aisee yaani hapa ninavyo piga ma self yaani rafiki zangu wana niaonea wivu balaa”

“Kuna maeneo ya humu ndani una ruhusiwa kupiga picha ila kuna maeneo baadhi ya hapa ikulu sio ruhusu kupiga picha hivyo utakapo zuiwa kupiga picha kwenye baadhi ya sehemu basi usishangae. Umenielewa?”

“Nimekuelewa shemeji”

Cauther akarudi sebleni hapa na moja kwa moja tukaongozana hadi katika eneo analo ishi raisi. Tukakuta wake wa viongozi mbalimbali wa kiserikali wakimfariji mke wa raisi.

“Eddy nataka kujua mume wangu alikufaje kufanye ikiwa wewe ndio ulikuwa na jukumu la kumlinda”

Mke wa raisi alipayuka huku akinifwata walinzi wangu walihitaji kumzuia ila nikawazuia wasimguse.

“Niambie mume wangu amekufaje kufanyeeeeee”

Mke wa raisi alizungumza hukua kinipiga piga kifuani. Nikamtazama Cauther ila akashindwa kufanya chochote zaidi ya kumuonea huruma mwanamke mwenzake.

“Usilete maigizo ikiwa una jua mpango mzima wa hawara wako makamu wa raisi. Na huyu alikuwa ni mume wako kwani alisha kupatia talaka. Sasa usitake nimwage mchele kwenye kuku wengi. Nina kupa ujumbe huu ukamfikishie changudoa mwenzako na umuambie kwamba nikimkamata, nita ufanya mwili wake chujio kwa maana si kwa risasi hizo nitakazo mpiga.”

Nilimnong’oneza mke wa raisi sikioni mwake na upuuzi wote alio kuwa ana ufanya kwa kuigiza ukamuisha na akatulia tuli na hata machozi yanayo mtoka kwa uwongo yakaanza kukatika taratibu usoni mwake.

“Na kitu kingine, mwanao akijua kwamba wewe una husika kwenye kifo cha baba yake basi naye ata kuchukia na uta mpoteza ni vyema ukakaa kimya na kuomboleza taratibu taratibu. Kwani nikuhitaji kukuchukulia sheria na wewe una kwenda na maji”

Nilizidi kumchimba biti mke wa raisi na akazidi kuwa mnyonge.Nikamuacha akiwa amesimama, nikawasalimia wake hawa wa viongozi wote, kisha nikamfwata Maria mtoto wa raisi, chumbani kwake.

“Hei Maria”

Nilizungumza huku nikikaa pembeni ya kitanda chake.

“Una jisikiaje?”

“Nahisi kuumwa Eddy”

“Pole nita muita daktari aje kukutazama”

“Amesha kuja na amesha ondoka. Eddy ni kuulize kitu?”

“Niulize”

“Kuna uhusiano gani kati ya mama na makamu wa raisi aliye ondoka madarakani?”

Swali la Maria likanifanya nivute pumzi taratibu na nikazishusha taratibu huku nikimtazama usoni mwake.

“Usinifiche hivi sasa mimi ni mtu mzima na nina elewa kila kitu. Hembu niambie kuna nini kati yao?”

“Kwa nini una uliza hivyo?”

Maria akanikabidhi simu yake na nikaanza kusoma picha(screen shot) za meseji ambazo zina onyesha ni mama yake ana chati na makamu wa raisi.

‘Hawezi kupona kabisa ile gesi iliyo fungwa ni kali sana’

‘Kwa hiyo nijiandae kupokea marehemu?’

‘Jiandae mke wangu kipenzi. Akifa tu nina kuoa na tuna rudi ikulu kwa mara nyingine’

‘Natamani afe hata sasa. Yaani nina mchukia sana yule mwanaume. Sijui ni mwanaume wa aina gani. Ehee Eddy naye ina kuwaje?’

‘Eddy huyo niachie mimi, ni paka niliye mlea mimi mwenyewe hivyo hawezi kunishinda kwa lolote lile najua wapi kwa kumshika, ata achia usukuni alio pewa ikiwa hajui njia’

‘Yaani baby nina kupenda hapo tu’

‘Ila nilitamani hichi kifo cha boya kitukute tuwe pamoja. Tusherekee kwa kupeana mechi kabambe’

‘Hahahaa, ila wewe mwanaume ni mtamu sana. Hapo ni uzeeni una nisugua kama hivi, kipindi ulivyokuwa kijanailikwaje?’

Makamu wa raisi akasindikiza meseji yake kwa vialama vya motomoto akimaanisha kwamba alikuwa ni wa moto sana.

Nikajikuta nikishika kichwa huku nikimtazama Maria usoni mwangu.

“Yaani mama yangu ana dirika kula njama ya kumuua baba. Haki y Mungu kwa hili siwezi kumsamehe hadi kufa kwangu. Nilikuwa nina mpenda sana baba mdogo makamu wa raisi kumbe ni mshenzi namna hii’

Maria alizungumza huku machozi yakimbubujika.

“Maria”

“Bee”

“Hawa watu ni watu hatari sana. Nina kuomba kwa sasa usiwaambie chochote. Hizi meseji nina jitumia, zitakuwa ni kama ushahidi huko mbeleni”

“Sawa Eddy. Ila sasa hivi wewe ndio raisi, nina kuomba ulipe kisasi kwa jili ya baba yangu”

“Usijali Maria. Sasa hivi kuwa makini na usifanye chochote kitu cha kuhusiana na hawa watu bila ya kuniomba ushauri. Kama aliweza kumuua mzee kwa ajili ya starehe zake. Hashindwi kukuua ili awe huru”

“Asante Eddy”

“Tuta onana kesho”

“Sawa Eddy”

Nikaachana Maria na tukaondoka na mke wangu na kurudi eneo tulilo pangiwa kwa muda. Majira ya saa mbili usiku rafiki zangu Akira na wezake wakafika ikulu hapa. Nikawatambulia katika familia yangu na kwa pamoja tukapata chakula cha usiku kisha wakaondoka na kurudi hotelini.

“Willy yupo wapi?”

“Alisha kwenda nyumbani kupumzika”

“Sawa Judy na wewe nenda kapumzike kesho asubuhi nina kuhiyaji hapa”

“Nashukuru sana kaka”

Judy akaondoka nyumbani hapa.

“Mume wangu, baba alinipigia simu mida fulani hivi akaniambia ukifika hapa Tanzania ana omba aweze kuzungumza na wewe”

“Sasa hivi ni saa tano usiku. Ngoja nimpigie simu”

Nikampigia simu baba yangu mkwe, kwa bahati nzuri akapokea.

“Shikamoo mzee”

“Marahaba. Pole sana Eddy kwa kumpoteza kiongozi”

“Ni pole yetu sote baba. Ila asante, nimepokea ujumbe wako kutoka kwa Cauther hapa”

“Ni kweli ila ina bidi tuweze kuonana uso kwa uso kwa ajili ya mazungumzo.”

“Kesho tuta oanana”

“Sawa”

“Usiku mwema na msalimie mama”

“Nashukuru sana na zime fika”

Nikakata simu, nikarudia kuzisoma meseji za mke wa raisi.

“Duniani kuna watu wa ajabu sana”

“Kina nani hao mume wangu”

“Wapuuzi puuzi tu. Twende tukalale mke wangu”

Nikambeba Cauyther na kuelekea naye ndani. Taratibu Cauther akaanza uchokozi wa chini chini,kutokana najua akianza uchokozi huu ana hitaji haki ya ndoa, nikaona sina haja ya kumnyima. Nikampa haki yake kwa mwendo wa taratibu hadi akaridhika na hakuchukua muda mrefu akapitiwa na usingizi mzito.

Maandalizi ya kitafia ya mazishi ya raisi yakazidi kupamba moto. Sio nchi yetu pekee ndio inayo omboleza msiba wa raisi, bali hata nchi nyingi ambazo maraisi wao walikufa kwenye mlipuko nao wana endelea kuomboleza huku kauli mbiu kubwa inayo endelea duninia mzima ina sema ‘DUNIA INALIA TUMEPOTEZA VIONGOZI MAHIRI’, huku picha za viongozi wote walio fariki siku hiyo akiwemo raisi wetu ikiwepo kwenye picha inayo zagaa kwenye mitandao mingi ya kijamii.

“Judy”

“Ndio mkuu”

“Unajua Mungu naye ana makusudi yake”

“Kivipi?”

“Lati juzi tungebaki pale ukumbini tunge kufa na sisi?”

“Yaani hata hili nilimuambia Willy jana akasema, kifo cha raisi wetu kilitokea kwa ajili ya kutuokoa sisi”

“Ni kweli aisee. Daa na nina imani walikuwa wame walenga watu wengi nasi tukiwemo ila ndio hivyo wakatukosa”

“Ila mkuu nina jiuliza hilo bomu liliingiaje ingiaje pale ikiwa ulinzi ulikuwa ni mkali kiasi kile”

“Adui ni adui. Wewe ukiwaza hivi naye habweteki, naye ana waza ni namna gani atakavyo fanya uhalifu. Hivyo mambo yana kwenda kama hivyo mdogo wangu”

“Ila Al-quida hili ndio anguko lao. Wana kwenda kupigwa sasa na dunia nzima na mbaya zaidi wamejitangaza kwamba wana husika. Yaani hadi huruma nina waonea”

“Hawawezi kuanguka”

“Kwa nini mkuu ikiwa wameua viongozi wa mataifa makubwa, ya kati na madogo duniani?”

“Al-quida na makundi ya ajabu ajabu ajabu kama Al-Shabab, haya ni matawi tu. Ila kuna mizizi wao ambao ndio una wapa nguvu. Wewe kwenye miaka yako yote au historia unayo ijua wewe, ulisha wahi kusikia Al-Shabab wamepindua serikali na kuchukua madaraka zaidi ya wao kuteka teka miji na si kwa kipindi kirefu”

“Sija wahi kusika hadi majuzi hapa”

“Ndio ujiulize, wamepata wapi nguvu. Nani yupo nyuma yao na nani amewasukuma. Ukisha jua hilo basi ujue vita ya kuwaangusha hao watu ni lazima ipigwe kwenye mizizi na shina sio kwenye matawi kama watu wa nje wanavyo ona”

“Una taka kuniambia Scorpion wana wadhamini haya makundi?”

“Asilimia mia moja na nime kuja kujua kwamba wana nguvu mara baada ya kulipua ule ukumbi. Viongozi wote walio kuwa kwenye listi ambayo makamu wa raisi alinipatia ili niwaue. Wamefia mule ndani, wale magwiji wenyewe wametoka na wapo hai kwa maana walikuwa wana jua ni nini kinacho kwenda kutokea”

“Aisee hivi yule mzee amepatia wapi nguvu ya kuwatawala watu wote hao na amekuwa na nguvu kubwa kiasi hicho?”

“Judy mimi na wewe sijui kwa maana yule mzee alinilea na akatufanya sisi ni silaha zake za kufanya kila tulicho tumwa ila baada ya kuchokwa wakapanga kutua kwa kutustukiza. Na sifahamu ni kwa nini hadi leo ameniacha hai kwani nilopo kuwa dereva taksi nilikuwa ninaishi maisha ya kawaida tu.”

“Ila kaka sasa hivi nchi yetu ina nguvu kuliko nchi zote dunian. Kwa nini tusipambane na hao Scorpion na tukaangusha chini na kuwasambaratisha. Tuna majasusi mahiri, tuna kila aina ya vitengo vya ulinzi kwa nini tusipambane nao kimya kimya?”

Judy alinishauri huku tukiwa katika ofisi ya raisi ya hapa ikulu, ikiwa leo ndio mara yangu ya kwanza kuanza kazi katika ofisi hii kama raisi wa muda.



“Judy mapambano na Scorpion ni sawa sawa na ndugu wa tumbo moja wakapigana. Hapo ni lazima mmoja ata muharibu mwezake. Makamu wa raisi ana ijua hii nchi vizuri sana. Wewe na mimi ana tujua vizuri sana na yeye ndio aliye tuunganisha hadi tukajuana. Nina imani una tambua hilo”

“Natambua.”

“Kama waliweza kulipua kisima cha kutengeza nyuklia na kudhuru baadhi ya watu. Niambie ni vitu vingapi ambavyo vita haribiwa. Isitoshe hatujui msaliti ni nani kati yetu kwa maana tuna weza kupanga na kila tulicho kipanga kina kwenda kuteketezwa”

“Ila mkuu hili jambo tuna shirikisha watu wachache”

“Sawa tuna shirikisha watu wachache. Je familia zetu tuna ziweka wapi. Kwa maana wakishindwa kuja dhidi yetu watakacho kitafuta mbadala ni familia na watu wetu wa karibu, je hapo tuna tokea wapi. Leo usikie Willy ameuwawa uta jisikiaje?”

“Mmm”

“Jibu ni kwamba uta jisikia vibaya. Hii vita sio nzuri, una jua nikimtazama mke wangu na mtoto aliye mbeba tumboni mwake, sitaki kuongeza hatari nyingine mbele yangu. Acha tu nimalize hizi siku nitafute kwa kuhema”

“Sawa mkuu ila sijisikii amani kuwaona wana endelea kudumu kwenye maisha yetu”

“Yataisha, una jua tujue mzizi wake upo wapi, ila tukisema tangalie matawi tuta feli. Matawi nina imani ni hawa makamu wa raisi ila mzizi upo sehemu na huo ndio ukikatwa matawi hayana ujanja”

“Ila makamu wa raisi ndio muanzilishi?”

“Najua hajaanza peke yake. Je hao alio anza nao ni kina nani?”

Mlango ukafunguliwa na akaingia Maria sekretari wa raisi aliye pita.

“Muheshimiwa baba yako mkwe amefika na yupo hapa ofisini kwangu ana hitaji kuzungumza na wewe”

“Mruhusu aingie”

“Mimi ngoja nitoke”

“Poa badae”

Judy na Maria wakatoka ndani hapa. Akaingia baba mkwe, nikanyanyuka na nikasalimiana naye huku nikimkaribisha kukaa kwenye sofa zilizopo ndani hapa.

“Kwa kweli maisha yana badilika kwa haraka sana. Hongera sana Eddy”

“Nashukuru sana mzee”

“Ila ofisi ime kupendeza?”

“Kiasi chake ila nina muda si mrefu nita kwenda kuikabidhi mikononi kwa wana siasa”

“Kwani huitaji kuendelea kuongoza hii nchi?”

“Sihitaji kwa kweli kwani hata huo uraisi wenyewe ume kuja kwa bahati mbaya kama ajali. Vipi uandaliwe kahawa”

“Usijali nilisha kunywa, Cauther alisha niandalia, hapa nime toka kumuona”

“Sawa sawa”

“Ahaa tuna weza kutembea tembea kwa maaa hizi kuta zina weza kuwa na masikio”

“Hakuna shaka”

Tukatoka ndani hapa na baba mkwe. Walinzi wangu wakatuzunguka.

“Aisee una lindwa sana”

“Natamani niwaambie waniache peke yangu ila siwezi kwani ndio utaratibu.”

Tukafika kwenye eneo la bustani kubwa, walinzi wakatawanyika kisha mimi na baba mkwe tukaa kwenye benchi lililo tengenezwa kwa chumba na mbao.

“Kilicho nileta hapa mwanangu ni kitu ambacho sio kizuri sana ila ina bidi nikizungumze”

Nikakaa vizuri huku nikimtazama baba mkwe.

“Nakusikiliza mzee”

“Nina kuomba sana na nipo chini ya miguu yako. Nina kuomba uachane na mwanangu Cauther”

Nikastuka sana hadi baba mkwe akatambua kwamba nime stuka.

“Tafadhali sana Eddy niachie mwanangu. Nina kuomba umuache na maisha yake arudi kwangu na tuishi maisha ya kawaida”

“Bila ya kukuvunjia heshima mzee. Akili yako ipo timamu kweli?”

“Nipo timamu na hapa nimesha toka kuongea na Cauther, nimemuambia adai talaka kwako. Ili tuachane na wewe”

Maneno ya baba mkwe yakanipandisha jazba hadi nikatamani nimzabe kofi moja takatifu ila nikajizuia tu kwa heshima ya ubaba mkwe.

“Nina mpenda sana mwanngu kuliko unavyo mpenda wewe. Mimi ndio niliye mlea toka amezaliwa na nina jua uchungu wake. Hivyo ninacho kihitaji ni hicho tu. Achana na mwanangu full stop”

Baba mkwe akasimama ila nikamzuia na nikamshika mkono na kumkalisha chini kwa nguvu na akapigiza makalio yake kwenye benchi hili.

“Nenda karudishe ujumbe kwa huyo aliye kushinikiza kwamba niachane na binti yako na umuambie kwamba mimi ni mwanaume mwenye sheria zangu na msisimamo wangu. Endapo akajaribu kuingilia familia yangu, akakutumia wewe eti kisa upo karibu na mimi, nina kuhakiishia mzee, nitawaua. Mimi ndio raisi wa jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na mimi ndio mume halali wa mtoto wako kwa ndoa ya kikristo na ndoa ya dini yako ya kiislamu hivyo basi. Kaa mbali na mimi, na usijaribu kurudi tena kwangu na ukanishauri kwa hili. Mwanao amebeba damu yangu. Usijaribu kumchanganya kwa upuuzi wako kama huu tena kwenye kipindi kama hichi nita kuvunja mzee. Umenielewa?”

Nilizungumza kwa sauti nzito na ya chini chini hadi baba mkwe akaanza kutemeka kwa woga kwa maana hakuna siku hata moja niliyo muongelesha kwa sauti na hasira kama hii.

“Umenielewa?”

“Nd…io”

“Potea na usirudi tena hapa ikulu”

Baba mkwe akasimama kwa haraka.

“Msindikizeni mzee hadi kwenye gari lake na aondoke hapa”

“Sawa muheshimiwa raisi”

Walinzi wangu wawili wakaondoka eneo hili na baba mkwe huku nikivua koti langu kwani kwa jinsi hasira ilivyo nipanda nahisi mwili wangu una nichemka. Moja kwa moja nikaelekea katika eneo tunalo ishi hapa ikulu.

“Dada yako yupo wapi?”

“Chumbani”

Nikapitiliza hadi chumbani. Nikamkuta Cauther akiwa amekaa juu ya kitanda huku akilia. Nikakaa pembeni yake na taratibu akanikumbatia.

“Mimi nakupenda wewe, siwezi kufanya upuuzi wowote alio zunguumza baba. Nina kupenda snaa Eddy wangu”

Cauther alizungumza huku akiendelea kunikumbatia na kulia.

“Kama walishindwa kutuachanisha kipindi mimi ni dereva taksi, hawawezi sasa hivi. Nita hakikisha nina fanya kila kitu una kuwa salama, wewe na mwanao. Umenielewa mke wangu”

“Ndio nime kuelewa baby”

“Nina kupenda sana”

“Nina kupenda pia mume wangu, sijui baba amepatwa na nini wakati alikuwa yupo vizuri”

“Msamehe”

“Ahaa…amenikera sana. Yaani nilicho mjibu sikutaraji kama ipo siku nita fungua kinywa changu na kumjibu baba yangu mzazi”

“Ume muambiaje?”

“Ahaa tuyaache hayo mume wangu. Ila kusema kweli moyo wangu ume chafuka. Naomba nikae peke yangu kwa muda mume wangu. Sahamani sana”

Nikamtazama Cauther machoni mwake, kisha taratibu nikamuachia.

“Sawa. Nina rudi ofisini”

“Poa mume wangu”

Nikanyanyuka na nikatoka ndani hapa.

“Nadia nifwate”

“Sawa shemeji”

Nikaongozana na Nadia hadi ofisini kwangu.

“Ime kuwaje?”

“Baba alikuja hapa, tukampokea vizuri na akatusifia sana. Ila kuna simu wakati tuna kaa na kuzungumza naye. Akawa ana jibu tu, ndio mkuu, ndio mkuu. Hadi tukashangaa kwa maana baba ni nadra sana kuzungumza kwa unyenyekevu wa namna ile na alionekana kama kuwa na woga fulani alipo kuwa ana zungumza na ile simu.”

Nadia akatulia kidogo kisha akaendelea kuzungumza.

“Mimi nilimuuliza baba hiyo simu mbona kama ime kuogopesaha. Alicho nijibu ni kwamba hainihusu na akamgeukia dada na kuanza kumueleza kwamba wewe sijui sio mtu salama kwa maisha yake. Kuwa na wewe ana weza kufa na akafikia kwenye pointi iliyo mkera dada”

“Point gani?”

“Ya kuomba talaka. Pale dada Cau alishindwa kujizuia hasira yake na ukitegemea hali aliyo kuwa nayo basi alimfokea sana baba na baba naye akafoka sana. Akataka kumpiga vibao dada ila niliingilia kati na akasema ana kuja kwako na ata hakikisha kwamba ndoo yenu ina vunjika kwa namna yoyote ile”

Nikamtazama Nadia usoni mwake.

“Toka ume nifahamu, kuna kosa lolote nililo mkosea mke wangu au familia yako?”

“Hapana”

“Ile ndoa waliyo andaa wazazi wako ilikuwa ni ya bahati mbaya au?”

“Walikusudia kabisa kufungisha ndoa yenu. Ila nahisi baba kuna kitu nyuma ya pazia ana tuficha. Ila shem nina kuhakikishia nita fanya upelelezi wagu hadi nitambue ni nani ambaye ana husika”

“Usijali wala usijisumbue”

“Hapana shemeji, ana mtia stress dada. Kwa hali yake ile huoni kama mimba yake ina weza kupata mushkeli kwa maana baba kumnyooshea kidole dada nakumbuka ni kipindi mimi nina miaka saba. Ila leo amenyooshea kidole tana akiwa mtu mzima na familia yake na isitoshe sehemu takatifu kama hapa ikulu. Lazima kutakuwa na jambo”

Mlango ukafunguliwa akaingia Willy.

“Ahaa samahani kaka tuna weza kupata hata dakika mbili”

“Ndio, Nadia kakae na dada yako na hakikisha kwamba chochote kitakacho tokea kwa dada yako una nijulisha”

“Sawa shemeji”

Nadia akatoka ndani hapa.

“Mkuu mtandaoni kume chafuka aisee”

“Kuna nini?”

“Kuna video clip ina sambaa ukimua mtoto mdogo kwa kumpiga risasi na imenadikwa kama raisi Eddy ana weza kmuua mtoto ata shindwaje kumuua raisi wake ili achukue madaraka”

Willy mara baada ya kuzungumza kanionyesha video hii. Nikakumbuka mtoto huyu nilimuua kwa kumpiga risasi ndani ya kitengo cha NSS, pale baba yake na mama yake tulipo wakamata na baba yake ndio ana husika na kifo cha Maulid na nina kumbuka siku hiyo nilishikwa na hasira sana hivyo ikanilazimu kuua familia nzima.

“Muheshimiwa hii ni ishu kubwa sana, wana nchi wengi wana kuja juu”

Judy naye akaingia kwa kasi.

“Mkuu umeiona video”

“Ndio, Judy una kumbuka kale katoto”

“Nakumbuka vizuri ila ile siku si kamera za kile chumba zilizimwa?”

“Ndio zilizimwa, sasa sijui ni nani alirekodi hili tukio”

Mshauri mkuu wa raisi naye akaingia hukua akiwa na simu yake. Kwa jinsi alivyo tukuta ina onyesha dhairi kwamba tuna jua kinacho endelea.

“Mkuu una weza kulitolea maelezo hili kwa maana vyombo vya habari vimeanza kuchachamaa”

Nikajikuta nikiinamisha kichwa chini kwani kisheria hata kwenye vita watoto huwa hawaruhusiwi kuuwawa labad itokee ajali ila hii ina onyesha kabisa nina mtazama mtoto huyu kisha nina mpiga risasi bila ya huruma.

“Muheshimiwa raisi tuna kusikiliza”

Mzee alizungumza huku akinitazama.

“Nani ameisambaza hiyo video?”

“Yaani kaka hata mimi sijui kwa mana ina ingia kama vile meseji. Haipo YouTube wala sehemu nyingine yoyote hapa ndipo mtihani ulipo”

Willy alizumgumza, nikatuliza akili kisha nikakumbuka hiyo siku makamu wa raisi alikuwepo.

“Najua aliye fanya hili ni nani?””

“Ni nani?”

Mshauri mkuu aliniuliza.

“Ni makamu wa raisi. Huyu jamaa na mke wake, walihusika na kifo cha kijana wangu yule Maulid tena usiku wa harusi yangu. Walimteka, wakampiga na ikawa ime salia kidogo tu wamue kwa risasi ila niliwawahi. Tukamkimbiza hospitalini na mimi nika wahi hawa watu kabla hawajatoka nchini Tanzania. Nilikuwa na dogo, tuliwapata pale aneo la Msata kitu kama hicho si hivyo Judy?”

“Ndio”

“Tuliwashambulia walinzi wake na kuwaua. Huyu jamaa na familia yake tukawatia mbaroni na kuwarudisha kitengo cha NSS. Oder niliyo pewa na raisi aliye pita ilikuwa ni kuwaua familia nzima. Nikiwa kama mwanajeshi ninacho fwata mimi ni oder nikaua na niliwaua nikiwa na hasira ya kijana wangu kutekwa na haikupita hata simu Maulid alikufa. Sasa sioni dhambi hapo kwa maana huyu mtoto na mama yake tunge waacha hai wange kwenda huko kujipanga na mwishowe wangerejea na kutudhuru ndio manaa tuliamua kukata mzizi wa ftina.”

Nilizungumza kwa msisitizo mkubwa sana.

“Basi kama ni hivyo muheshimiwa raisi ina bidi tulitafutie ufafanuzi wa haraka. Kumbuka bado hatujamzika raisi aliye pita. Linakuja hili, huoni kuta kuwa na hali mbaya siku ya msiba wa mzee?”

Mshauri wa raisi alizungumza.

“Ni kweli muheshimiwa, ina bidi tupate ufafanuzi”

“Nina weza kui modify hii video ikanoekana kama editing hivi”

Willy alizungumza.

“Kivipi?”

“Yaani pale si una onekana ni wewe. Basi tuna tafuta hata kichwa cha gaidi gani huko tuna kiweka na tuna waonyesha watu na kuwatolea ufafanuzi kwamba aliye fanya tukio pale sio wewe ni mtu mwengine”

“Kama ina wezekana kijana fanya hivyo”

“Willy”

“Ndio kaka”

“Fanya hivyo”

“Ila jamani ngojeni. Walio fanya hili jambo wana onekana ni watu walio jipanga sana kwa maana hii video imeingia tukwenye simu yangu. Hakuna namba wala link iliyo ingiza hii video. Ina onekana wana utaalamu wa hali ya juu sana kwneye teknolojia ndio maana ime sambaa kwa haraka. Endapo tukitoa video feki kwamba sio raisi hapa, alafu na wao wakatoa ufafanuzi, huoni ni tuna muweka raisi hatarinizaidi ya hapa?”

Ushauri wa Judy ukatufanya sisi sote kukaa kimya huku tukitafakari cha kufanya.

“Hilo nalo neno”

Nilizungumza kwa sauti ya unyonge.

“Muheshimiwa raisi kikubwa hapa sio wewe kukimbia tatizo wala kulifunika funika tatizo na lisionekane kuwa ni tatizo. Wewe kuwa muwazi kwa raia. Waambie kila ukweli wa siku hiyo ulivyo tokea, watakao kuelewa acha wakuelewa na wasio kuelewa acha wasikuelewe ila ukweli upo nje. Kama alivyo sema binti hapa. Tukisema tulifunike funike hili jambo mwishowe lita fumuka kubwa zaidi ya hili”

Mashauri wa raisi alizungumza kwa upole huku akinitazama machoni mwangu. Nikaa kimya kama dakika tano huku nikijashauri kichwani mwangu na kuwatazama wote watatu.

“Itisheni mkutano na waandishi wa habari”

“Hapana hatuhitaji waandishi wa habari kwenye hili mkuu. Uta toa ufafanuzi wewe kama wewe na baada ya hapo tuta angalia ni namna gani wananchi watakavyo lipokea kisha ndio tuta amua tukae chini na waandishi wa habari au laa”

Mshauri mkuu wa raisi alizungumza.

“Sawa nime kuelewa mzee. Si nina kwenda mubashara?”

“Ndio”

“Sawa andaeni nizungumze”

“Hakuna shaka muheshimiwa raisi”

Mzee akatoka ndani hapa na nikabaki na Willy pamoja na Judy.

“Ndio maana nilisema hichi kiti sikitaki. Ninavyo ona makaburi yanaanza kuchimbuliwa.”

“Aisee, mmm hadi nimeanza kuogopa kwa kweli”

“Ndio maana nilikuambia Judy hii miezi iksha ni vyema tukaachana na hizi kazi. Mambo mengine nilawama kwa watu wenye uelewa mfupi”

“Yaani raia kwenye mtandao wa kijamii wana tokwa na povu balaa”

Willy alizungumza na kunifanya nitabasamu kidogo. Mshauri wa raisi akaingia ndani hapa

“Muheshimiwa raisi kila kitu tayari una dakika tano za kujiandaa”

“Sawa”

“Huandikiwi sehemu?”

Willy aliuliza huku akinitazama.

“Usijali dogo nina kwenda kuzungumza mimi mwenyewe kitakacho nitoka kama kita kuwa ni kizuri au kibaya. Mungu pekee ndio anaye jua na sija waomba kura hawa wananchi hivyo wasiniumize kichwa mimi”

Maneno yangu yakamfanya Willy kuguna kwa maana nimeyazungumza kibabe sana. Nikasimama, nikavaa koti langu la suti na tukatoka ofisini hapa, tayari kwa mimi kwenda kupambana na fukuto linalo endelea kwenye mitandao ya kijamii huko.



“Ina bidi upakwe make up muheshimiwa raisi”

Mmoja wa wahusika wa hahabari alizungu huku akinitazama usoni mwangu.

“Hakuna haja kwa maana sio mahojiano”

Nikasimama eneo ninalo paswa kusimama nikahesabiwa hadi tatu kisha nikaanza kuzungumza.

“Ndugu Watanzania wezangu, ni matumaini yangu mu wazima wa afya. Katika kipindi hichi kigumu cha kuondokwa na raisi wetu mpendwa. Zimezuka kasfa na shutuma zidi yangu na zikionyesha video ya mimi nikimuua kijana mdogo kwa kumpiga risasi”

Nikanyamaza kwa sekunde kadhaa kisha nikaendelea.

“Ndio mimi nilimuua. Na nilifanya tukio hilo kwa sababu baba yake alikuwa ni gaidi. Gaidi aliye ua vijana wangu wa kazi. Gaidi aliye husika kuondoa watu muhimu kwenye muhimili wa kazi. Nina imani wananchi wengi wata kuwa wana jiuliza, kundi la X la kwanza lilikwenda wapi? Wezangu watatu nilio kuwa nao waliuwawa kikatili huku mimi nikiponea chupuchupu kwa kupigwa risasi kadhaa mwilini mwangu.”

“Mission yangu ilikuwa ni kuhakikisha na mimi nina lipa kutokana na damu za ndugu zangu zilizo mwagika. Hawakuishia hapo, nilipo unda kundi la X jipya munalo liona kwa sasa, wakamuua kijana wangu anaye itwa Maulid, kikatili sana, walimtesa, wakampiga na nilimuokoa na akafia hospitali. Maulid ni baba na ana ndugu wanao mtegemea. Alikuwa kijana wa miaka ishirini na nane tu, ila ndoto zake za kutumikia hili taifa zilizimwa na watu wanao endelea kutuwinda roho zetu.”

“Wananchi muna ishi kwa kula, kunywa na starehe ila kuna watu wana ishi kwa ajili ya kuwafanya nyinyi hizo starehe zenu zisiwe na bugudha. Kama hamuamini hilo angalieni nchi kama Somalia. Angalieni nchi kama Iraq na nyinginezo ambazo watu hawana hata muda wa kwenda kanisani wala misikitini.”

“Gaidi hapaswi kuishi yeye na familia yake. Haijalishi ni mtoto ana umri mmoja, mwezi au miaka. Kwa maana endapo tukimuacha ata turudi na akiturudi ata tudhuru na akitudhuru nyinyi wananchi ndio mutateseka. Sijutii kuiangamiza ile familia na wala sijasimama hapa kuomba msahama dunia au mtu. Leo hii raisi wetu ameuwawa kwa kuwekewa sumu ya gesi. Anatokea mpuuzi ana dai kwamba mimi ndio nime muua kwa sababu ya madaraka. Sipo hapa kwa ajili ya kuhitaji hichi kiti cha uraisi. Nita iongoza nchi kwa miezi husika kama katiba inavyo dai na sinto gombania uraisi kwani sijaumbwa kuwa raisi. Nime umbwa kuwa mpiganaji, na katika kupigana kuua sio dhambi kwani nisipo ua basi nita uliwa mimi. Hivyo ni vyema nyinyi munao endelea kunishambulia kwa maneno kwenye mitandao ya kijamii muelewe kwamba tuna fanya kwa ajili ya nyinyi kuweka makalio yenu majumbani, maofisini na sehemu nyigine zote bila ya kuwa na mawazo ya aina yoyote ile.”

“Watu waliuwawa uwanja wa ndege, wakubwa kwa watoto. Nani alilalamika, nilikwenda kuyaweka maisha yangu reheni na vijana wangu kwa ajili ya kuwatoa wale watu salama na kuwaangamiza wale watekaji. Mulicho ishia ni kusifa na kutazama video clip za jinsi tunavyo fanya, tunavyo hatarisha pumzi zetu. Tuna penda kuishi, nina familia, nina mke ninaye mpenda. Ila ana elewa nini nina fanya. Hivyo basi, nikiwa kama raisi, sinto hitaji wala sita taka kusikia au kuona video hiyo ikiendelea kujadiliwa. Endapo uta fanya hivyo basi uta kumbana na matatizo. Nchi sasa hivi haiongozwi na mwana siasa atakaye waambia uongo. Nchi ina ongozwa na jeshi hadi pale raisi atakapo patikana hivyo musitochokoze”

Nilizungumza kwa kujiamini na watu wote ndani ya chumba hichi wana nishangaa, nikamuona Willy akiwa amefumba macho kwa maana hichi nilicho kizungumza sio nilicho andikiwa kukiongea.

“Niliishi kwa kupewa amri na niliteleza amri kama jinsi makamu wa raisi aliye pita alivyo niamuru kuia hiyo familia. Niwatakie siku njema”

Nikaondoka eneo hili kisha nikaanza kutembea kuelekea ofisini kwangu huku Judy na wezake wakinifwata nyuma. Nikaka kwenye kiti hichi cha kuzunguka na nikawatazama washauri wangu.

“Nini?”

Niliwauliza huku nikiwakazia macho.

“Samahani muheshimiwa raisi. Kile ulicho kizungumza pale ni kosa la kidemokrasia kwa maana wananchi wana haki ya kuzungumza kile wanacho jisikia?”

Mshauri mkuu wa raisi alizungumza.

“Sio kwenye kila kitu. Ndio maana jeshi halifungamani na raia na vitu vya jeshi havijadiliwi na raia kama wanavyo jadili maswala ya mpira au hizi siasa za kipumbavu”

Nilizungumza kwa kufoka hadi nikamuona mzee akitemeka kwa kuogopa kwa maana kichwa kimesha vurugwa.

“Wasubiri nitoke madarakani kisha ndio waongee upuuzi. Mimi kusema kweli sina moyo wa kusemwa na nikakaa kimya. Haki ya Mungu watu watekwenda kupiga kwata ili wajue mateso tunayo yapitia. Tuna elewana mzee wangu?”

“Ndio muheshimiwa raisi”

“Naombeni mutupishe”

Judy alizungumza kwa sauti ya upole na watu wote wakatoka ndani hapa na nikabaki naye.

“Eddy, najua uma gadhibishwa na hili lililo tokea hapa. Ila tambua kwamba ume kosea”

Nikamtazama Judy kwa macho makali na yaliyo jaa hasira ila hakuniogopa wala kutetereka.

“Raisi ni mtu ambaye ni wajuu sana katika nchi. Tusema ni baba kwenye familia ya watoto wengi sana. Kuna watoto ambao ni waelewa, wasio kuwa waelewa, wakorofi, wafwata mkumbo na kadhalika. Endapo baba ata toa hali ya vitisho kwenye hiyo familia. Wapo watakao furahia, chukia na kuchukulia poa.”

“Najua kweli oparesheni za kijeshi hazipaswi kujadiliwa na wananchi. Ila kumbuka ile video ilikuwa ni ya wewe kwend akuitolea melezo na kuwaomba msamaha wananchi basi inge isha. Ila hivi ulivyo kwenda kujikweza na kuwachimba mkwara na kutaka kutumia jeshi kama sehemu ya kuwatisha wananchi. Nisikufiche umekosea kaka yangu na unapo kosea ni lazima nikuambie ukweli unao kuuma ili siku nyingine usikosee”

Maneno ya Judy yakapenya hadi moyoni mwangu na kujikuta machozi yakinilenga lenga.

“Haya ni maisha kaka yana isha muda na wakati wowote. Juzi juzi tu raisi Alen alikuwa amekalia hicho kiti ila leo yupo kwenye friji Mochwari akisubiria siku yake ya kuzikwa. Jaribu kujua busara na hekima ni ngao kubwa sana kwa adui kama makamu wa raisi.”

“Ila si nimesema oder nimepewa na yeye?”

“Hilo ndio ume liongea kaka je swala wananchi kuwatishia wasizungumze chochote”

“Wanaongea nini Judy ehee au kwa sababu wewe huonekani pale?”

Nilizungumza kwa ukali.

“Hata niongeonekana Eddy ila hili swala lina swala ungeliua kiustarabu. Hata wale walio sambaza hiyo video wangethayari. Ila kipo wapi eheee?”

Judy naye alikuja juu.

“Sizungumzi kama nazungumza na raisi nina zungumza na zaidi ya mtu wangu wa karibu. Kaka ambaye alijitoa maisha yake kwa ajili ya kutuokoa sisi. Nina tambua thamani yako ndio maana sitaki thamani yako ipotee. Umenielewa. Nataka ukitoka kwenye hicho kiti uishi maisha ya kuheshimiwa huko mitaani na sio maisha ya kuogopewa. Kumbuka hilo kaka”

Judy alizidi kuzungumza kwa msisitizo. Nikashusha pumzi taratibu huku nikiendelea kumtazama Judy machoni mwake.

“Naomba password yako ya Twitter?”

“Ya nini?”

“Nahitaji kuwaomba radhi wananchi kwa hili ulilo zungumza ila nitaandika kama wewe ndio uliye andika kwa maana kuna muda na wakati inabidi usaidiwe”

Nikaendelea kumtazama Judy kwa sekunde kadhaa kisha nikamtajia namba za siri za akaunti yangu ya Twitter. Akaanza kuandika ujumbe wa kuomba msamaha wananchi.

“Baba mkwe ana nizingua”

Judy akanitazama na hakujibu chochote zaidi ya kuendelea kuandika.

“Tayari nimesha post. Una weza kuingia kwenye akaunti yako uka soma”

“Badae”

“Ume sema baba yako mkwe ana kuzingua na nini?”

“Ameniambia nimpatie mwanaye talaka na amemuambia Shamsa adai talaka kwangu”

Nilizungumza kwa upole huku asira ikiwa tayari imesha katika.

“He!! Amechanganyikiwa au?”

“Hata sielewi aise, ila nahisi hawa walio sambaza video ndio walio mshinikiza”

“Ila si uliniambia baba mkwe wako naye yupo huko kwenye scorpion?”

“Ndio, na nilikuwa nina mtumia yeye kama mpelelezi wangu ila naona sasa nime pata hii nafasi hivyo wana mpelekesha. Yaani mambo yana pandana sana ndugu yangu”

“Kaka”

“Naam”

“Usiwaze hilo jambo ni upuuzi kwani nina imani mke wako hawezi kukubaliana na hilo”

“Yaa amekataa kabisa”

“Basi achana na hizo mambo. Jambo la msingi ni wewe kuangalia hii miezi iliyo salia tuna imaliza vipi na hali ya wifi ina endeleaje, si una tambua kwamba hapaswi kuwa na mawazo ya mara kwa mara na makubwa kama hayo?”

“Yaa natambua”

“Hivyo hakikisha huruhusu kabisa hayo mawazo.”

Judy alizungumza kwa sauti ya upole”

“Sawa nashukuru rafiki yangu. Maandalizi ya mazishi yamefikia wapi?”

“Yamekamilika kwa asilimia tisini na nane, kesho kutwa tuna zika”

“Sawa nita shukuru hili nalo likiisha”

“Sawa kaka. Ume choka nenda kapumzike”

“Nashukuru”

Nikasimama na kuanza kutembea taratibu kuelekea mlangoni. Kabla sija fungua nikageuka na kumtazama Judy.

“Judy asante”

“Asante ya nini muheshimiwa raisi?”

“Kwa kila kitu”

“Usijali”

Nikatabasamu kisha nikatoka ndani hapa. Walinzi wakanisindikiza hadi nyumbani kwangu, nikawakuta Nadia na dada yake wakiwa sebleni, Cauther akataka kunyuka ili anipokee ila nikamzuia ake tu kwenye sofa. Nikamfwata alipo kaa na nikambusu katika lipsi zake kisha nikakaa pembeni yake.

“Pole mume wangu”

“Nashukuru sana, kichwa kime vurugika balaa”

“Najua hilo mume wangu, hukuzungumza vile kwa kupenda ni hasira ya maudhi ya baba”

“Shem pole”

“Asante shem. Vipi mke wangu mawazo yamepungua?”

“Kiasi chake”

“Usijaribu kuwaza sana na hilo jambo. Angalia afya yako na afya ya mtoto tumboni. Ukifanya hivyo mambo yana weza kuwa mabaya. Umenielewa mke wangu”

“Ndio baba watoto. Nikupikie nini?”

“Leo nahitaji shemeji apike”

“Sawa shem mimi nipo tayari. Una taka kula nini mume”

Nadia alizungumza huku akiwa amejawa na furaha kubwa sana.

“Nahitaji kula samaki wa kukaanga, kachumbari na ugali wa kutosha”

“Sawa mume, ngoja nikaandae mambo jikoni”

“Vipi shem umesha zoea huko jikoni?”

“Sana yaani. Kama kwangu vile”

Nadia akaondoka na kutuacha sebleni.

“Ehee niambie mume wangu?”

“Yaani kuongoza nchi ni balaa tupu. Nimeikumbuka sana nyumba, haya maisha ya kufwata fwata na walinzi kama mkia yaani mimi siyawezi”

“Yaani hata mimi nime choka mume wangu. Kazi ni kukaa ndani kama utumbo. Ukitaka kutoka hata uende matembezi, yaani hadi ujulikane ni wapi una taka kwenda uongozane na walinzi”

“Hahaa pole mke wangu, nimekuingiza kwenye maisha ambayo siyo”

“Yaani wee acha tu mume wangu. Mama alinipigia simu nikazungumza naye. Akasema kwamba baba kuna watu wamemtishia hivyo akashinikizwa kuja kuzungumza yale maneno, hivyo ana tuomba radhi sana kwa kia kilicho tokea”

“Usijali nili elewa kwani mzee sio aina ile ya watu”

“Ni kweli, hata mimi mwenyewe awali nilihisi utani utani ila alipo kuwa ana zidi kuzungumza nikatambua kwamba ishu alikuwa ana maanisha.”

“Mambo ya mpito tu hayo”

Nadia akamaliza kupika chakula na kwa pamoja tukala kisha mimi na mke wangu tukaingia chumbani kulala.

“Nimepitia pitia huku kwenye mitandao naona ume kuwa gumzo sana”

Cauther alizungumza huku akitandika kitanda vizuri.

“Wana semaje?”

“Wapo wana kusifu kwa uhodari wako na wapo wana lalamika kwa kauli zako. Ila mume wangu usijali maneno ya watu wewe fanya kile unacho hisi ni bora kwa ajili ya hii nchi”

“Nashukuru mke wangu kwa kunielewa. Ukinielewa wewe tu ina tosha”

Simu yangu ikaanza kuita, nikaitazama na kuona private namba ambayo kwa mara nyingi makamu wa raisi ndio anaye itumia.

“Mbona hupokei simu mume wangu”

“Ni makamu wa raisi”

“Mpokelee labda ana hitaji kukuambia jambo la maana”

“Ahaa….ana taka kunivuruga akili yangu”

“Wewe poke tu mume wagu”

Nikapokea simu hii na kuiweka sikioni huku nikiyafumba macho yangu kwani nina jua atakacho kizungumza makamu wa raisi hapa kita nivuruga tu.

“Hahaa aaa ume utupia mpira kwangu ehee?”

“Hivi wewe mzee huwa una kosa kazi ya kufanya. Hembu niache basi na maisha yangu. Sitaki kukutukana”

“Mara ngapi ume nitukana. Eddy…..Subiria nita kupatia suprize yako moja kubwa sanaa na huto amini”

“Nenda zako nimesha kuzoea maneno maneno yako hayo”

“Eti ehee?”

“Mzee hembu niache nilale”

“Una taka kulala?”

“Nataka kuamka, mpuuzi wewe”

“Eddy nisikilize nina kitu chako cha thamani kuliko hata huyo mke wako. Endapo uta kubali tubadilishane na nafasi ya uraisi basi uta kipta kitu hich ila ukikataa basi huto kipata milele daima”

“Kitu au mtu wa thamani ni mke wangu na mwanangu anaye zaliwa. Hivyo sina haja ya kelele nyingi”

“Jidanganye”

Nikakata simu na kuizima kabisa.

“Pole mume wangu, nimekulazimisha kupokea simu kumbe ita kukera”

“Aha…nimesha zoea”

Tukapanda kitandani huku mawazo ya kitu cha thamani alicho kuwa ana kizungumza makamu wa raisi yakijirudia kichwani mwangu mara kwa mara.

‘Ni kitu gani?’

Nilijiuliza ila nikaosa jibu hadi usingizi ukanipitia. Nikasikia mlango ukigongwa, nikafumbua macho yangu na tayari mwanga wa jua umetawala ndani hapa. Nikashuka kitandani, nikavaa pensi na kufungu mlango.

“Za asubuhi muheshimiwa raisi”

Mshauri mkuu wa raisi alizungumza huku akinitazama machoni mwangu.

“Salama shikamoo”

“Marahaba. Nime jaribu kupiga simu yako mara nyingi ila haipo hewani”

“Nilizima jana usiku”

“Sawa, muheshimiwa raisi una hitajika commanding room kuna tatizo”

“Najitayarisha nina kuja sasa hivi”

Nikafunga mlango na kukimbilia bafuni, nikaoga haraka haraka na nikavaa moja ya suti na yote yakiendelea Cauther bado yupo usingizini. Nikambusu shavuni mwake kisha nikatoka ndani hapa na kuongozana na mshauri wangu mkuu.

“Ehee niambie kuna tatizo gani?”

Nilimuuliza mzee huyu huku tukitembea kwa hatua za haraka katika kordo hii ndefu huku mbele wakiwa wametangulia walinzi wawili na nyuma wakiwa walinzi wawili.

“Kuna habari tume ipoke asubuhi hii kutoka vyombo vya hali ya hewa wana sema katika masaa machache yajayo hali ya hewa ina weza kuwa hatari zaidi sana.”

Tukaingia katika ukumbi huu na watu wote wakasimama. Nikawapa ishara ya kukaa.

“Muheshimiwa raisi karibu. Mimi ni Jonathan ni mkuu wa kitengo cha hali ya hewa hapa nchini”

“Nashukuru kukufahamu bwana Jonathan. Ehee nipe taarifa ni nini kinacho kwenda kutokea”

“Muheshimiwa raisi nina masikitiko kukuambia kwamba kuna uwezekano wa hali ya juu Tsunami kutokea leo majira ya kuanzia saa nane usiku na kuendelea hii ni kutokana na vipimo vyetu vinavyo onyesha hali inayo kuja”

Macho yakanitoka huku nikiwa nimeshikwa na bumbuwazi kwani hili janga la Sunami halizuiliki na kwa miaka kadhaa tulishuhudia jinsi lilivyo leta maafa makubwa katika nchi Indonesia, Sri Lanka na India, huku Tanzania, Kenya, Somalia na Afrika kusini nazo zikiwa katika mkumbo wa wimbi hilo kubwa la bahari.



Nikatazama video inayo onekana kwenye screen kubwa ya tv jinsi tetemeko hilo la ardhi linavyo anza taratibu na lina kutanuka basi lita sababisha volcano kufumuka na ikifumuka basi wimbi kubwa lina weza kutokea na kusababisha maafa.

“Hakuna njia na namna ya kulizuia kwa maana kesho kubwa ndio mazishi ya raisi aliye pita?”

“Haiwezekani mkuu, hivyo ina bidi serikali iweze kutangaza hali ya hatari kwa watu walio katika fukwe za bahari mikoa kama ya Dar es Salaam, Tanga, Mtwara. Zanzibar waweza kutafuna namna ya kuhama ili kuepusha maafa makubwa sana”

“Ila muda ulio salia hapa muna jua ni mchache. Masaa kumi na saba sio rahisi kuhamisha watu”

Nilizungumza huku nikiwatazama watu wote ndani hapa.

“Ni kweli muheshimiwa raisi ila ni bora nusu shari kuliko shari kamili”

“Nahitaji kupiga simu”

Nilizungumza huku nikisimama. Nikaingia kwenye moja ya chumba cha vioo, nikatoa simu yangu mfukoni na kumtafuta mchungaji ninaye muamini.

“Mchungaji ni mimi”

“Ohoo asante Mungu, nina ona mwenyezi Mungua ameamua kutimiza maono yake ndani ya muda mfupi sasa”

“Nisikilize mtumishi. Nina kuomba upige goti kumuomba Mungu azuie hili linalo kwenda kutokea”

“Kuna nini tena?”

“Kuna Tsunami ina weza ikatoka hivyo nina kuomba sana tena sana uweka timu yako ya maombi na iweze kuomba leo siku nzima kwani hiyo ndio njia pekee ya kuzuia jambo hilo. Umenielewa mchungaji”

“Nimekuelewa na nina ingia magotini mwa bwana. Hatato kufa ila tuna ishi kwa imani”

“Amen”

Nikakata simu na kushusha pumzi, nikaitafuta namba ya mzee na kumpigia. Simu yake ikaanza kuita hadi ikakatika, nikapiga kwa mara ya pili na akapokea.

“Ndio Eddy”

“Mzee wangu heshima yako”

“Nashukuru sana”

“Mzee wangu kuna jambo lina kwenda kutoka. Vyombo vyetu vya hali ya hewa vina onyesha dalili kwamba kuta kuwa na Tsunami inayo weza kutokea majira ya saa nane usiku hivyo una weza kuangalia kwenye mitambo yako?”

“Mmmm hakuna kitu kama hicho, kinge kuwepo ningekiona siku nyingi na ninge kueleza”

“Ila mzee wangu mbona ya mzee kuuwawa hukuniambia?”

“Ila kuna mtu alikuambia, na ulimshauri ila alikataa si ndio?”

“Ndio”

“Basi kilicho muua ni ubishi wake na laiti angekubali na angerudi basi hadi leo hii angekuwa bado yupo hai”

“Kwa hiyo una taka kuniambia Tsunami haipo?”

“Hakuna Tsunami wala kitu chochote”

“Sasa ni nini walicho kiona”

“Ipo hivi kuna mtua na hitaji ufanye makosa na uonekane muongo na upoteze uaminifu na wananchi wakuchukie na wajutie kuongozwa na mtu kama wewe hivyo tuliza akili mjukuu wangu.”

“Sawa mzee”

Nikakata simu huku nikishusha pumzi, nikatazama watu jinsi wanavyo endelea kuzunguka zunguka huku hofu zikiwa zimewajaa kwa maana hakuna anaye tamani kufa. Nikatoka ofisini hapa na kukaa kwenye kiti changu, ukimya ukatawala huku nikitazama watu wote humu ndani.

“Muheshimiwa ina bidi utangaze hali ya hatari na watu waanze kuondoka mjini hapa”

“Hakuna kitu kama hicho. Nahitaji uchunguzi ufanyike tena juu ya hicho kitu. Hatuwezi nchi kama nchi kuingia garama ambazo ni za kukadirika. Nchi kama Marekani na wengine wangekuwa wamesha liangaza hilo. Chunguzeni tena”

Watu wote wakatazamana huku kila mmoja akiwa haamini juu ya maamuzi yangu.

“Tumeelewana?”

“Ndio muheshimiwa raisi”

“Nahitaji vipimo vyenu sasa hivi vichukuliwe na Satelite, muna masaa mawili ila kwa sasa siwezi kutoa tamko lolote kwa wananchi. Asanteni”

Baada ya kuzungumza maneno hayo nikasimama na watu wote wakasimama na nikatoka ndani hapa. Moja kwa moja nikaelekea hadi ofisini kwangu.

“Muheshimiwa raisi una jua masaa mawili ni mengi sana ina kupasa uangalie na hali halisi inayo kwenda kutokea”

Mshauri wangu alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.

“Judy na wengine wapo wapi?”

“Bado hawajafika mkuu”

“Sawa”

“Ila muheshimiwa kama unavyo ona ina bidi uhame ikulu hii na kuelekea ikulu ya Dododoma kwa muda hadi hili swala tukitazamia jinsi linavyo kuwa”

“Mzee wangu nikuulize jambo?”

“Bila shaka”

“Una ogopa kufa eheee?”

Swali langu kidogo likaleta kigugumizi kwa mzee huyu, akanitazama pasipo kunipa jibu lolote.

“Nakuuliza una ogopa kufa?”

“Kila bina damu ana hofu na kifo”

“Basi nina kuruhusu uweze kuchukua mapumziko ya wiki moja. Nenda mbali kabisa na Dar es Salaam nina imani uta kuwa salama huko uendapo. Sawa mzee wangu”

“I…la muheshimiwa hii ilikuwa kwa ajili ya usalama wako?”

“Mke wangu yupo hapa. Ana mimba yangu ila mbona sijapanic na kutaka kukimbia mji. Acha tuone nini kitatokea”

“Sawa”

Mlango ukagongwa na Judy akachungulia. Nikamuita kwa ishara na wakaingia yeye na Willy, tukasalimiana nao.

“Tuna habari njema muheshimiwa”

Judy alizungumza.

“Habari gani?”

“Mzee alinipigia simu akanieleza kitu ambacho mkuu wa hali ya hewa alikiona. Willy aliweza kufanya kazi ya kutazama kama kwenye miamba ya bahari kuna weza kutokea hali yoyote hatarishi ila kila kitu kipo shwari kabisa”

Macho yangu yakamtazama mzee huyu.

“Kaka hii ndio hali ya hewa ilivyo, Hii ni level ya kwanza ya habari na hii ni core ya mwisho kabisa ambapo ndipo kuna volcano. Hivyo katika zone ya Tanzania na Afrika kwa ujumla na hata hapa katikati kwenye mabara mengine hakuna hali yoyote ya kutisha. Kila kitu kipo salama kaka”

Willy alizungumza huku akinielekea kupitia video yake.

“Mzee mpigie simu yule mkuu wa idara ya hali ya hewa aje hapa ofisini”

“Sawa muheshimiwa raisi”

Mzee akaanza kupiga hatua kuelekea mlangoni.

“Vipi mzee una kwenda wapi. Mpigie hapa hapa”

Ikambidi mzee kurudi hapa hapa na akapiga simu mkuu wa idara ya hali ya hewa. Baada ya dakika tano akaingia mkuu huyo nikamsalimia na nikamribisha kwenye sofa.

“Ehee hembu niaambie ripoti yenu inaonyesha vipi?”

“Ile ya kwanza ua hii ya pili?”

“Kwani ya pili imesha toka?”

“Ndio ina shuhulikiwa?”

“Je ina mabadiliko?”

“Haina mabadiliko mkuu”

“Hembu niambie hii ya kwanza mume itoa wapi?”

“Hii ya kwanza muheshimiwa raisi imetokana nayo kwa vipimo vyetu”

“Willy hembu muelezee”

Willy akaanza kumueleze mkuu huyu wa idara ya hali ya hewa mbinu na namza yake alivyo tumia na kupima.

“Umeelewa mkuu”

Nilimuuliza mkuu huyu kitengo cha hali ya hewa,

“Ndio muheshimiwa raisi. Tungependa tukaungane na kijana huyu kwenye huu uchunguzi wa pili”

“Sawa mupo huru kuungana naye”

Willy na kiongozi wa idara ya maji wakaondoka ndani hapa.

“Mzee wangu nakumbuka nilikuruhusu ukapumzike”

“Muheshimiwa raisi nita endelea kufanya kazi”

“Hofu imeondoka?”

“Ndio mkuu”

“Nashukuru”

Mzee huyu akatoka ndani hapa na kutuacha wawili.

“Gody yupo wapi jamani simuoni”

“Yupo kwake na demu wake yule”

“Hivi alisha nunua nyumba?”

“Ndio maeneo ya mbezi Luis”

“Ahaa. Hivi ikitokea kweli Tsunami ina kuwaje?”

“Sidhani kaka kama ina weza kutoka”

“Yaani ndio ime tokea tuna fanyaje kwa maana tume kataa”

“Mmm hata sijui”

Simu yangu ikaanza kuita, nikaitoa katika mfuko wa suti na nikaona namba makamu wa raisi.

“Naona makamu wa raisi ana nizoea sasa”

“Kwa nini kaka?”

“Naona pigo zake sizielewi elewi kila siku ana nipigia simu na kunizingua zingua”

“Mpokelee na umsikie anacho kizungumza”

Nikapokea simu na kuiweka loud speaker ili sote tumsikie.

“Umeuruka mtego wangu ehee?”

“Una maanisha nini?”

“Maana yangu ni kwamba nilihitaji uonekane ni mtu usio na msimamo ndio maana nikaingiza taarifa feki kuhusiana na Tsunami.”

“Hahaahahaa, aisee mzee una zeeka vibaya, hivi kwenye hilo kundi lako la Scorpion hakuna washauri wa kukushauri”

Nilizungumza kwa dharuau ya hali ya juu.

“Ninao na mshauri mmoja wapo ni mama yako mzazi”

Tukatazamana na Judy, huku nikistuka kidogo.

“Sina mama mimi na alisha kufa miaka mingi”

“Eddy, Eddy, Eddy. Nimekuita mara tatu, mama yako yupo hai kama huamini nina kutumia picha zake sasa hivi ili umjue”

Makamu wa raisi akakata simu na kunifanya nishushe pumzi nyingi taratibu huku nikimtazama Judy usoni mwake. Baada ya muda mfupi picha nyingi zikaanza kuingia kwenye simu yangu, nikazifungua na macho yaanitoka kwani mwana mama huyu ana fanania kabisa na mimi.

“Mkuu vipi?”

Judy aliniuliza huku akinitazama.

“Hembu njoo uone”

Judy akanisogela, nikamuonyesha picha hizi na yeye akastuka kidogo huku akinitazama mara kadhaa na akatazama picha hizi.

“Hivi huwa ina wezekana mtoto akafanana sana na mama yake?”

“Ndio hususani watoto wengi wa kiume huwa wana fanana na mama zao”

“Ila miaka yote alikuwa wapi huyu mama hadi akanionyesha sasa hivi?”

“Mkuu huyu mtu ana kuchezea akili. Siku hizi kuna mambo mengi sana ana weza kuwa ametengenezewa sura ya bandia ambayo ina endana na wewe kabisa na akakudanganya kwamba ni mama yako”

Simu yangu ikaita na nikaiokea namba hii ya makamu wa raisi.

“Ehee”

“Naamini ume muona mama yako”

“Ndio”

“Nita kuja naye kesho kutwa kwenye msiba wa ndugu yangu. Hivyo endapo uta jaribu kunigusa, au kunidhuru basi nita muua”

Makamu wa raisi akashusha pumzi, nikamtazama Judy ambaye amesikia kila kitu.

“Asitumie udhaifu huu kukufanya umuogope mkuu. Hii ndio nafasi ya pekee ya kumkamata makamu wa raisi na kumfikisha katika vyombo vya sheria”

“Yule mzee sio mjinga na hakuna mahakama inayo weza kumfunga”

“Una maanisha nini?”

“Mzee ana nguvu kubwa Judy, kumkamata kwake ita kuwa ni moja ya anguko kubwa sana la hii nchi. Kitu kikubwa ambacho kilikosewa sana na viongozi wa kipindi chake ni kumfanya huyu mzee kama muhimili mkubwa wa mambo mengi hususani uchumi ndio maana una weza kumuona ana jiamini na ana fanya kila ancho kiweza”

“Ina maana mkuu na wewe umesha muogopa?”

“Simuogopi ndio maana huwa nina jibizana naye kwa kila jambo. Ila nina ogopa maisha ya watu wengine, kwa nini watu waumie kwa ajili yangu. Hili swala tuliache kama lilivyo, acha nimalize hizi siku niondoke kwa usalama. Huyo nitakaye muachia madaraka ata jua namna gani ya kuongoza nchi. Sitaki vifo vitokanavyo na mambo ya ajabu”

Nilizungumza huku nikinyanyuka.

“Sawa mkuu”

“Acha nikanywe chai, nina njaa”

Nikatoka ndani hapa na kurudi ninapo ishi, nikawakuta Cauther na mdogo wake wakiwa wamekaa sebleni. Nikasalimiana nao kisha Cauther akaniandalia chai.

“Mke wangu hembu tazama picha za huyu mwana mama”

Nilizungumza huku nikimkabidhi Cauther simu yangu.

“Hee ni nani huyu mbona una fanana naye mume wangu!?”

“Yaani wee acha tu”

“Hembu nione dada”

Cauther akampatia simu Nadia.

“Kweli shem una fanana naye. Ni mama yako kwani?”

“Inavyo sadikika”

“Kusema kweli una fanana naye mume wangu. Ila nani kakutumia picha?”

“Makamu wa raisi”

“Mmmm kazitoa wapi?”

“Sijajua ila ameniambia siku ya mazishi ya muheshimiwa ana kuja naye”

“Aisee una fanana naye sana, aje tumuone mama mkwe”

Cauther alizungumza kwa furaha sana. Mara baada ya kumaliza kunywa chai nikarudi ofisini na nikaletewa ripoti ya pili juu ya hali ya hewa.

“Mkuu tumedhibitisha kwamba ripoti ya kwanza iliweza kuchezewa hivyo hakuna Tsunami”

Mkuu wa kitengo cha hali ya hewa alidhibitisha hilo.

“Nashukuru kwa hilo”

Nikaendelea na majukumu ya kawaida ya kiofisi hadi muda wa kuondoka ofisini kwangu ulipo wadia. Huku nikipokea salamu za rambi rambi kutoka kwa mataifa mengine juu ya msiba raisi wetu huku nami nikituma salamu za rambirambi kwa nchi zote zilizo ondokewa na maraisi wao na zenye urafiki na nchi ya Tanzania

***

*******************************************************************

Ili uwe wa kwanza kupata episode za mbele za hadithi hii kabambe ya X unacho paswa kufanya ni kuwasiliana nami whatsapp 0742334453 au 0657072588. Kama upo Facebook uta ipata kupitia facebook inbox kwenye page yangu ya Story Za Eddy-tz .EPISODE MOJA NI SH 250/= TU. Wahi sasa

*********************************************************************

Siku ya kuuaga ramsi mwili wa raisi ukawadia. Shehere za kuuga mwili wake zikafanyika katika uwanja wa Taifa huku mimi nikiongoza taratibu za kuuga mwili wake kabla ya kupelekwa mkoani Tabora kwa ajili ya mazishi vijijini kwao. Wananchi wengi sana wamekusanyika uwanjani hapa huku vilio vikitanda kila sehemu. Nikamtazama makamu wa raisi kwa jicho kali huku akiwa amekaa kwenye jukwaa la viongozi.

Taratibu za mazishi zikaanza huku zikiongozwa kwa dini ya kikristo.

Nikamtazama mke wa raisi, jinsi anavyo jifanya ana lia kwa uchungu nika jikuta nikichukizwa na namna anavyo igiza. Nikamtazama mtoto wa raisi Maria, nikamuona akiwa amekaa mbali kidogo na kiti cha mama yake.

“Muheshimiwa mtoto wa raisi ana hitaji kuzungumza”

Nilinong’onezwa na Judy kwa maana katika ratiba mtu aliye paswa kuzungumza ni mke wa marehemu na sio Maria.

“Sawa”

Judy akamnong’oneza muongoza shuhuli hii na baada ya muda kidogo Maria akaitwa, akasimama akiwa na mlinzi wake wa kike. Akatembea kwa kujiamini hadi kwenye jukwaa la kuzungumzia. Akawekewa maiki vizuri na kwa kimo chake. Akajifuta machozi yanayo mchuruzika kwa uchungu hadi nami nikajikuta machozi yakinilenga lenga.

“Baba alikuwa ni mtu jasiri sana. Baba alikuwa ni mwanaume ambaye ana simama kwenye misingi na taratibu anazo ziamini kuhakikisha yale anayo yaamini yana kwenda kukamilika. Baba yangu alikuwa ni kiongozi wa kweli. Baba yangu alikuwa ni mtu wa kweli, sio muongo wala mlaghai.”

Nilishangazwa na ujasiri unao uonyesha Maria.

“Ujasiri na umahiri wa baba uliwafaya maadui zake kuanza kunyanyuka. Maadui ambao walikuwa wapo tayari kuhakikisha wana fanya kila liwezekanalo wana muangamiza baba yangu. Usiku ambao baba yangu alipanga kuuwawa nilikutana naye na niliongea naye mambo mengi sana. Baba nakumbuka aliniambia jambo moja. Mtu pekee wa kumuamini ni Eddy. Eddy ambaye ameyatoa maisha yake yote kuhakikisha ana mlinda baba yangu. Akaniambia hata mama yako usimuamini, kwa mara ya kwanza nilishindwa kumuelewa kwa nini nisimuamini mama ila sasa nina elewa”

‘Ohoo Mungu wangu mtoto ana kwenda kumwaga mchele kwenye kuku wengi’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikiwa nimejawa na wasiwasi kiasi cha kutamani kuomba Maria ashushwe ila ndio hivyo tayari yupo mbele ya macho ya watu wanao taka kusikia ni kwa nini hamuamini mama yake.



“Mama nina kuchukia sana, mama haiwezekani ukala njama kubwa kama hii. Kama watu wote hawajui basi leo hii nina zungumza ukweli. Mama na makamu wa raisi aliye stafu wana mahusiano ya kimapenzi na wao ndio wamehusika na kifo cha baba”

Karibia uwanja mzima ukajawa na mshangao.

“Ushahidi nipo nao”

Maria alizidi kuzungumza kwa ujasiri na uchungu wa hali ya juu. Nikakaagiza mara moja walinzi waweze kumzunguka Maria ili amalizie kuzungumza anacho jisikia kukizungumza. Nikamtazama makamu wa raisi na kumuona jinsi macho yanavyo mtoka kwa mshangao. Nikamuona mke wa raisi akianguka na kuzimia, watu wa huduma ya kwanza kwa haraka waka mshuhulikia.

“Baba yangu ameuwawa kwa kuwekewa hewa ya gesi chumbani kwake. Makamu wa raisi na mama ndio walipanga hilo jambo ili kumuua baba ili waendelee na mapenzi yao na makamu wa raisi aje kuwa raisi wa hapo baadae”

”Muheshimiwa raisi tufanyaje?”

Mlinzi wangu namba moja alininong’oneza sikioni mwangu.

“Hakikisheni makamu wa raisi na mke wa raisi wana shilikiwa na wakahojiwe juu ya hili”

”Sawa muheshimiwa raisi”

Amri yangu ikatekelezwa mara moja makamu wa raisi, akaondolewa uwanjani hapa kwa ulinzi mkali huku gari ya wagonjwa iliyo mbebea mke wa raisi nayo ikilindwa kwa ulinzi mkali.

“Muheshimiwa raisi wa sasa nina kuomba haki itendeka haijalishi alikuwa ni mama yangu au alikuwa makamu wa raisi haki ifwate mwenendo wake. Nina shukuru”

Maria akanifwata hadi kwenye kiti nilicho kaa, akanikumbatia kwa muda.

“Ume fanya jambo ambalo sikutarajia kabisa kama unge weza kulifanya”

“Nilikuambia Eddy ila sikuona hatua yoyote uliyo chukua. Ndio maana nime jitoa sadaka najua wata niwinda na kuniua, ila bora nife ila ukweli nime sema. Na siwezi kuona adui zangu wana leta maigizo mbele ya marehebu baba yangu”

“Sawa kuanzia hivi sasa uta kuwa katika ulinzi maalumu. Ume nielewa”

“Sawa Eddy”

Maria akarudi katika kiti chake huku utaratibu wa kumlinda ukiwa umebadilika.

“Mmmm mume wangu hii ni hatari aliyo itafuta Maria”

Cauther alininong’oneza.

“Yaani hapa amemwaga mchele mbele ya kuku wengi”

“Mmmm kazi kweli kweli”

Muda wangu wa kuzungumza ukafika, nikaelekea katika eneo zilipo maiki huku walinzi wangu wakiendelea kunilinda kwa umakini sana.

“Bwana Yesu asifiwe”

“Amen”

“Tumsifu Yesu Kristo”

“Milele amen”

“Ndugu zangu wa Tanzania. Taifa lime pata pigo moja kubwa, pigo la kuondokewa na kiongozi mwenye msimamo na aliye jenga misingi bora kwa watu wake hadi mtoto wake. Kiongozi ambaye hakuogopa kufa kwa ajili ya watu wake. Kikubwa alicho kihitaji ni kuona watu wake wana fanikiwa na wana fika katika safari ambayo amekusudia wafike”

“Namkumbuka raisi wangu kama mtu ambaye alihakikisha kwamba nchi kwanza na maslahi yake binafsi ndio maana mumeona kwenye kipindi cha uraisi wake watu wengi ambao hakupenda wawe na nguvu kuliko sheria. Walijitahidi kuhakikisha wana mdhuru kwa namna mbalimbali kikwemo na kuvamia viwanja vya ndege na maeneo mbalimbali.Ili kumshinikiza afanye kama vile wanavyo hitaji afanye”

“Raisi aliicha nchi ikwia katika hali ya uhitaji wake, kuanzia uongozi hadi mawazo yake. Nimekabidhiwa jukumu ambalo hata siku moja sikuwahi kuliwaza au kuliota kama nita kuja kukutana nalo.”

“Ila kutokana niliumbwa kuwa tayari kwa kila jambo na muda wowote basi nipende kuwahakikishia wananchi kwamba nipo tayari. Nchi itakuwa salama hadi pale muda wangu utakapo kwisha”

“Alilo lizungumza Maria mtoto wa raisi, nikiwa kama kiongozi wa nchi nitalifanyia kazi na sheria ita fwata mkondo wake, haijalishi ni nani au alikuwa nani amehusika katika hili na nina imani kwamba sheria ya nchi yetu ikimkuta mtu na hatia ya mauaji basi kuna adhabu mbili, kifungo cha maisha au kunyongwa hadi kufa kabisa. Basi musishangae mahakama ikafanya maamuzi hayo kwa walio tajwa kwa maana mamilioni ya Watanzania walihakikisha wanamchagua kiongozi na akatangazwa kuwa raisi. Ila kwa tamaa za watu wachache na ushawishi mbaya waka taka kufanya kile walicho kifanya. Haiwezekani na haivumiliki na niwaambie tu ukweli, ushahidi nime uona na una dhibitisha hilo na utafanyiwa kazi”

“Nitoe onyo kwa yoyote, au kikundi chochote cha uhalifu, kinacho tarajia au kupanga kumuua Maria, kisa kuzungumza ukweli hadharani. Niwaahidi, nitavua suti yangu na nita weka pembeni na nita wasaka kama mwanajeshi, kwani kiti changu ya uraisi hakibadilishi uwezo wangu wa ufanyaji wa kazi na hakibadilishi uzalendo wangu juu ya nchi yangu. Ifikie hatua nchi iongozwe kwa misingi na taratibu za kisheria na si kwa matakwa ya mtu yoyote wala kikundi chochote eti kisa tu waliwekeza au walisaidia mambo fulani ndani ya nchi yakaenda vizuri”

Wananchi walio hudhuria hapa uwanjani wakapiga makofi kunipongeza.

“Nichukue tena fursa hii kuwaeleza wale wote mulio husika kwenye tukio la kulipua chungu cha nyuklia na baadhi ya ndugu zetu wakapoteza maisha kutokana na sumu kali. Niwaambie ukweli, faili lenu nimesha lipata na lipo mezani kwangu. Ipo hivi, hatuto wakamata hata mmoja, ila tuta wapoteza kama mulivyo poteza ndugu zetu na kutia hasara kubwa taifa letu. Nikizungumza nita wapoteza nina imani jeshi na vyombo vingine za ulinzi muna nielewa”

Wananachi wakasahau kama wapo msibani wakapiga makofi kwa shangwe.

*******************************************************************

Ili uwe wa kwanza kupata episode za mbele za hadithi hii kabambe ya X unacho paswa kufanya ni kuwasiliana nami whatsapp 0742334453 au 0657072588. Kama upo Facebook uta ipata kupitia facebook inbox kwenye page yangu ya Story Za Eddy-tz .EPISODE MOJA NI SH 250/= TU. Wahi sasa

*********************************************************************

“Tume choka kuona damu za ndugu zeti zikimwagika kama machinjio ya ng’ombe. Niwahakikishie tu kwa kipindi changu cha hii miezi kadhaa niliyo pewa kwa mujibu wa katiba na sheria ya jamuhuri ya Muungano wa Tanzania. Maeneo makubwa ya miji na sehemu mbalimbali za nchi, wanajeshi wangu watiifu wata saidiana na askari kwa ulinzi wa raisi na nchi kwa ujumla. Tupo kazini na hatuto lala wala hatuto fumba mboni za macho yetu hadi pale tunaye msaka atakapo anguka chini”

“Nenda kwa amani raisi wangu, nenda kwa amani mpambanaji mwenzangu. Nenda kwa amani mkuu wa majeshi wangu. Umeacha vyuma na tuta simama kwenye misingi yako. Mungu ailaze vyema roho yamarehemu amen”

Nikapiga satuli ya ukakamavu na nilipo anza kurudi kwenye kiti changu wananchi wote wakasimama na kuanza kunishangilia. Wingi wa watu walio hudhuria humu hakika wame badilisha hali fulani katika moyo wangu. Hali ya wasiwasi kuhisi kwamba wananchi wana nichukia ila leo naona mambo yamekuwa tofauti. Nikapeana mikono na viongozi kadhaa kisha nikakaa kwenye kiti changu. Cauther aliye kaa mkono wangu wa kulia, taratibu akanishika kiganja changu.

“Nina jivunia na kuwa na mwanaume kama wewe”

Cauther alininong’oneza.

“Nashukuru mke wangu”

Ukawadia muda wa kuimba wimbo wa taifa. Watu wote tuka simama na tukaanza kuimba wimbo wa taifa. Baada ya wimbo wa taifa kuisha, tukaketi na ukawadia muda wa sisi kuuga mwili wa raisi, nikaanza mimi na mke wangu kisha tukatoka uwanjani hapa na kuingia katika gari la raisi na moja kwa moja safari ya kueleeka uwanja wa ndege kupanda helicopter maalumu ya raisi ambayo ina uwezo wa kutua sehemu yoyote ukawadia.

“Sikuwahi kuota kama nita ishi maisha haya ya kusindikizwa na ving’ora namna hii”

Cauther alizungumza huku akitazama jinsi pikipiki za askari wa usalama barabarani jinsi walivyo lizunguka gari letu.

“Umeyapenda?”

“Kiasi chake ila sio sana”

“Hahaa ila nita fwata kile unacho kihitaji sinto kuwa raisi tena baada ya hapa”

“Sawa mume wangu”

Tukafika uwanja wa ndege, mimi na mke wangu tukaingia katika helicopter maalumu ya raisi ambayo kwa Tanzania tuna ita The One. Helicopter hii ime undwa maalumu kwa ajili ya kumbeba raisi kwa safari zote za ndani ya nchi, kama ana kwenda mikoa ambayo ni ngumu kwa ndege ya raisi kutua kwenye viwanja kutokana na ukubwa wake. Sifa ya helicopter hii haiwezi kushambuliwa angani kwani ina uwezo wa kujilinda yenyewe. Mshauri wangu mkuu, Judy na Willy nao wakaingia ndani ya helicopter hii pamoja na walinzi wangu wawili na taratibu safari ya kuondoka eneo hili ikaanza huku helicopter nyingine mbili zinazo fanania na hii zikaanza kupaa sambamba na helicopter hii.

“Maria yupo wapi?”

“Amepanda helicopter ile kule”

Judy alinijibu huku tukitazamaa helicopter iliyo kaa upande wa hukushoto huku helicopter nyingine ikiwa upande wetu wa kulia.

“Okay mke na makamu wa raisi wapo wapi?”

“Wapo kitengo cha NSS wamewekwa chini ya ulinzi”

“Washenzi sana”

“Kumbe yule mzee ni mtu mbaya ehee?”

Cauther alizungumza.

“Ndio hivyo mke wangu”

Tukafika mkoani Tabora na moja kwa moja tukaelekea kijijini kwa raisi na tukakuta ulinzi ume imarika kisawa sawa.

“Aisee mzee amejenga sana”

Nilizungumza huku nikitazama majumba mazuri ya kifahari yaliyo jengwa kijijini hapa.

“Amewajengea watu wake”

“Yahaa”

Moja kwa moja tukaelekea katika nyumba ya wana familia na tukawapa pole kisha tukajumuika nao kuusubiria mwili wa raisi ambao una letwa kwa helicopter ya jeshi. Baada ya nusu saa helicopter ya jeshi ikatua eneo hili. Vilio vya wana ndugu na wananchi wa kijiji hichi zikaanza kutawala mara baada ya jeneza la raisi kushushwa kwenye ndege huku likiwa limefunikwa bendera ya Tanzania. Jeneza likaingizwa katika chumba maalumu kilicho andaliwa kabla ya taratibu za kuuaga na kuuzika hazijaanza. Saa yangu ya mkononi ina onyesha sasa hivi ni saa nane mchana na msiba uta anza kufanyika saa kumi jioni.

Taratibu zote za maziko zikaanza kufnayika huku ibada ikiongozwa na baba askafo mkuu wa dhebebu la kanisa la KKKT. Si wamama na wasichana wanao lia, hadi hadi watoto na vijana, kwa kweli raisi alitengeneza upendo mkubwa kwa watu wake. Baadhi ya watu wanashindwa kuhimili majonzi haya na wana zimia. Kusema kweli nime udhuria misiba mingi ila msiba huu kusema kweli ume tikisa taifa na taifa lina omboleza kisawa sawa.

“Maria yupo wapi?”

Nilimuuliza mlinzi wangu.

*******************************************************************

Ili uwe wa kwanza kupata episode za mbele za hadithi hii kabambe ya X unacho paswa kufanya ni kuwasiliana nami whatsapp 0742334453 au 0657072588. Kama upo Facebook uta ipata kupitia facebook inbox kwenye page yangu ya Story Za Eddy-tz .EPISODE MOJA NI SH 250/= TU. Wahi sasa

*********************************************************************

“Yupo kwenye chumba ulipo hifadhiwa mwili”

“Nahitaji kwenda kumuona”

Nikanyanyuka kwenye eneo nililo kaa na moja kwa moja nikaelekea katika chumba hichi. Walinzi wakabaki nje na nikaingia ndani hapa na kumuona Maria akiwa amekaa pembeni ya jeneza la baba yake huku likiwa limefunguliwa eneo la kuanzia kifuani mwake hadi usoni mwake. Tararibu nikakaa pembeni ya Maria huku sote tukiutazama uso wa raisi, kwa namna alivyo lala una weza kusema ni mtu ambaye ata amka muda wowote.

“Eddy”

“Naam”

“Neno la mwisho baba kukuambia lilikuwa ni nini?”

Maria alizungumza kwa sauti ya kawaida kabisa kama hakuna kilicho tokea.

“Nilizungumza naye mambo mengi sana kabla hajakufa”

“Je una jua juu ya mahusiano kati ya makamu wa raisi na mama yangu?”

“Ndio na alimpa talaka mama yako siku moja kabla ya sisi kuelekea nchini Ujerumani”

Maria akanitazama kwa macho makali kidogo kisha akamtazama baba yake.

“Baba alinipenda sana kuliko mama sijui kwa nini?”

Nikakosa cha kuchangia kwenye hili.

“Eddy”

“Naam”

“Ikitokea mtu akamuua mtu umpendaye hususani mke wako uta mfanya nini?”

Swali la Maria likanifanya nishushe pumzi taratibu huku nikimtazama usoni mwake.

“Nita fanya kila liwezekano kuhakikisha nina lipa kisasi”

“Kama?”

“Kumuua”

Maria akanitazama kwa sekunde kadhaa kisha akaka kimya kwa dakika moja.

“Una weza kunifundisha”

“Kukufundisha nini?”

“Kumuua mtu na kutumia silaha”

Ombi la Maria likanifanya kukaa kimya kwa muda.

“Una taka kumuua nani?”

“Mama na makamu wa raisi. Hawastahili kuishi, wameniulia baba yangu nao wana paswa kufa”

“Maria, kumua mzazi wako ni laana?”

“Laaana, Eddy leo hii una sema ni laana kumuua mzazi wangu. Hakuna kitu kama hicho. Yeye amemuua baba hajapata laana. Eddy lazima niwaue tu”

Maria alizungumza kwa msisitozo huku machozi yakimlenga lenga.

“Usijali sheria ita chukua mkondo wake”

“Sinto jali swala la sheria ila nita waua, Eddy ukubali au usikubali ni lazima ni waue hata kama kwa kuwatuma watu kwa kuwalipa nita waua tu”

Simu yangu ikaingia ujumbe mfupi, nikaitoa mfukoni na kuusoma ujumbe huu.

“SAHAU KUMUONA MAMA YAKO MZAZI, KWA HILI UTA JUTA”

Ujumbe huu una toka kwa makamu wa raisi jambo ambalo likanifanya nistuke kidogo, Judy akaingia ndani hapa na moja kwa moja akanifwata na kuninong’oneza sikioni mwangu.

“Muheshimiwa kuna tatizo nina kuomba mara moja”

Nikanyanyuka na tukatoka ndani hapa pasipo hata kumuaga Maria.

“Kuna nini?”

“Makamu wa raisi na mke wa raisi wame potea katika kitengo cha NSS katika mazingira ya kutatanisha”

“Nini?”

“Ndio muheshimiwa”

“Mkuu wao yupo wapi?”

“Naye yupo hapa msibani na kule alibaki msaidizi wake”

“Wameuwawa au?”

“Hata sijui muheshimiwa raisi ila hicho kitu ndio nime ambiwa sasa hivi”

“Hichi kitengo ni cha kipuuzi sana. Ina kuwaje wana muachia mtu muhimu kama huyo. Au wamesha leta usaliti wao?”

“Sifahamu muheshimiwa”

“Muite mkuu wao nina hiyaji kumuona sasa hivi”

“Sawa muheshimiwa”

Nikahisi kichwa kikipata moto. Baada ya dakika tano mkuu wa kitengo cha NSS akanifwata sehemu nilipo simama huku wakiwa wameongozana na Judy.

“Imekuwaje?”

“Muheshimiwa raisi hadi sasa hivi tupo gizani. Mfumo mzima wa NSS ume fungwa na hapa ninavyo zungumza ni kijana wangu mmoja amenitumia video hii, ikionyesha jinsi mauaji yanavyo endelea ndani ya jengo la NSS”

Caro akanionyesha video iliyo rekodiwa kwa kuyumba yumba jinsi askari wake wakiuwawa kwa kupigwa risasi na watu walio valia suti nyeusi.

“Shitii umetumiwa muda gani?”

“Kama dakika kumi au saba zilizo pita muheshimiwa raisi”

“Nahitaji mipaka viwanja vya ndege bandarini na sehemu nyingine zote msakako mkali ufanyike. Tuna elewana?”

“Ndio muheshimi raisi”

“Wasilianeni na jeshi na hakikisheni kwamba jeshi lina ishuhulikia hii oparesheni”

“Vipi muheshimiwa raisi niingie kazini?”

Judy aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.

“Nakuhitaji karibu yangu. Acha wapo wa kushuhulikia”

Simu yangu ikaanza kuita. Nikaitoa mfukoni na kuona private namba ambayo nina amini ana itumia makamu wa raisi. Nikaipokea simu hii na kuweka loud speaker.

“Eddy usisumbuke kunitafuta kwa maana nimesha ondoka nchini Tanzania muda mrefu sana. Ila kwa hili ulilo lifanya wewe na huyo mpuuzi mwenzako lita yagarimu maisha yenu nyote wawili. Bye”

Makamu wa raisi akakata simu na kinifanya mimi na Judy pamoja na Caro tutazamane kwa maana kama ameweza kutoroshwa ndani ya muda mfupi tu basi hali zetu nazo zipo hatarini hususani familia zetu.



“Hivi huyu mzee amechanganyikiwa ehe?”

Caro aliuliza huku uso wake ukiwa umejawa na hasira. Nikakunja ngumi huku nikiwa nimepandwa na jazba isiyo ya kawaida sana.

“Niiitie Willy”

“Sawa”

Judy akaondoka na kuniacha na Caro. Baada ya muda Willy akafika hapa.

“Umesikia kilicho tokea dogo?”

“Judy ndio ana niambia sasa hivi aisee”

“Kwa ujuzi ulio upata kwa Wajapan una weza kunitafutia makamu wa raisi kupitia hizo satelaite zenu?”

“Ndio”

“Fanya hivyo”

“Sawa kaka”

“Nita hakikisha nina muwinda na kumuua kwa mikono yangu huyu mzee siwezi kusumbuliwa na mpumbavu mmoja”

Nilizungumza huku nikijitahidi kuizuia hasira yangu hapa msibani kwa maana waandishi wa vyombo vya habari ni wengi sana. Muda wa mazishi ukawadia, taratibu na heshima zote za maziko juu ya raisi yoyote zikafanyika ipasavyo. Kutokana nilisha ongea Dar es Salaam hapakuwa na haja ya mimi kuzungumza tena msibani hapa.

“Mimi nina rudi Dar es Salaam leo. Nina imani uta kuwa mkakamavu”

Nilimuambia Maria mtoto wa raisi mara baada ya mazishi haya kuisha na baadhi ya watu kutawanyika na kwenda kuendelea na kazi zao.

“Nita kaa hapa kwa siku mbili na baada ya hapo nina hitaji kurudi ikulu kuzungumza kile nilicho kizungumza na pia nita hitaji kuonana na mama kabla sijamuondoa duniani”

Nikatoa simu yangu kwenye koti la suti yangu na kumuonyesha video fupi ya jinsi makamu wa raisi alivyo fanya umaafa kwenye kitengo cha NSS kisha akatoroka na mama yake.

“Hadi hapa ninavyo zungumza mama yako hatupo naye mikononi mwetu. Wametoroka ndio maana nina rudi leo Dar es Salaam”

“Shiti…..tuna ondoka wote Eddy, sina haja ya kubaki hapa”

Maria alizungumza kwa msisitozo na kunifanya nimtazame usoni mwake kwa sekunde kadhaa kisha nikatingisha kichwa nikimaanisha nime mkubalia tuondoke pamoja. Nikawaaga ndugu wa karibu wa raisi kisha tukaanza safari ya kuondoka eneo hili. Ukimya ukatawala ndani ya helicopter hii huku kwa mara kadhaa nikimtazama Maria jinsi anavyo tazama nje ya kioo cha helicopter hii. Cauther taratibu akanishika kiganda cha mkono wangu wa kulia.

“Muheshimiwa raisi”

Mshauri wangu aliniita.

“Ndio”

“Kuna simu yako hapa?”

Nikachukua simu hii maalumu ambayo huitumia raisi kwenye mazungumzo ya kiserikali kwani ni moja ya simu ambayo mazungumzo yake hayarekodiwi na mtandao wowote wa simu.

“Imetokea wapi?”

“North Korea”

Nikaipokea na kuiweka sikoni mwangu.

“Raisi Tanzania”

“Eddy habari yako”

“Salam asana muheshimiwa raisi habari za siku nyingi”

“Nina mshukuru Mungu muheshimiwa raisi, vipi North Korea?”

“Salama, nime ona hali iliyo tokea kwa kweli kutoka moyoni mwangu nina kutakia pole sana”

“Nina shukuru sana muheshimiwa raisi.”

“Hawa washenzi walio husika na kifo cha raisi wenu pamoja na maraisi wengine mume panga kuwafanya nini nyinyi kama nchi”

*******************************************************************

Ili uwe wa kwanza kupata episode za mbele za hadithi hii kabambe ya X unacho paswa kufanya ni kuwasiliana nami whatsapp 0742334453 au 0657072588. Kama upo Facebook uta ipata kupitia facebook inbox kwenye page yangu ya Story Za Eddy-tz .EPISODE MOJA NI SH 250/= TU. Wahi sasa

*********************************************************************

“Muheshimiwa raisi hadi sasa hivi bado sija tengeneza mfumo wa kudili na hao watu. Ila kuna watu zaidi ambao tuna paswa kudili nao. Hao ni matawi, kwenye mti ukikata matawi sio njia ya kuudhohofisha mti kwa maana mti una weza kuchipua matawi. Kilicho salia sasa hivi ni kukata mzizi hilo ndio ninalo liwaza”

“Ukihitaji msaada wowote kutoka kwangu usisite kuniambia, laiti kama wangeua hata mkorea mmoja wa kaskazini. Nina kuhakikishia ninge waua asubuhi yake. Ila hawakujichanganya kwenye hilo, nina hitaji uwe mahiri kuliko ulivyo kuwa awali. Nina kujua na nina amini kwenye uwezo wako Eddy”

“Nashukuru sana muheshimiwa raisi kwa kunipa moyo”

“Sikupi moyo, nina hitaji usimame imara. Una ongoza taifa kubwa, taifa lenye uchumi mkubwa na silaha kubwa, hakikisha una kuwa mairi”

“Nime kuelewa muheshimiwa raisi nashukuru sana kwa hilo na nita fanya”

“Muda wowote ukinihitaji wasiliana nami”

“Sawa muheshimiwa raisi”

“Siku njema”

“Nawe pia”

Nikakata simu mara baada ya kuzungumza na raisi wa Korea Kaskazini. Raisi ambaye kipindi nipo na kundi langu la X aliweza kutusaidia kwenye mambo mengi ikiwemo mafunzo mbalimbali ya kujiimarisha na kutufanya tuzidi kuwa kundi bora na kundi linalo ogopewa sana. Tukafika ikulu, mimi na washauri wangu tukaingia kwenye magari ya msafara na kueleka katika kitengo cha NSS huku mke wangu pamoja na Maria tukiwaacha hapa. Tukafika katika kitengo hichi na kukuta wanajeshi wakiwa tayari wameumarisha ulinzi.

“Karibu muheshimiwa raisi nina itwa Kanali Edern”

Mzee mmoja alinisalimia mara baada ya kunipigia saluti.

“Nashukuru kukufahamu. Kuna madhara gani yaliyo tokea?”

“Ni ambush muheshimiwa raisi, wana usalama zaidi ya thelathini na sita wameuwawa. Kuna mabomu yalitegwa kwenye jengo hili ndio maana wengi waliweza kufariki”

Nikatazama uharibifu wa majengo haya ya kitengo cha NSS. Nikahisi kama moyo una taka unichomoka kwa maumivu na hasira kali niliyo nayo.

“Hakuna hata mvamizi mmoja aliye kamatwa?”

“Hakuna muheshimiwa raisi”

Nikazunguka karibia eneo zima la kitengo hichi cha NSS, nikisaidiana na mkuu wao Caro. Baada ya kuzunguka na kukagua uharibifu wote ulio fanyika, nikarudi ikulu na washauri wangu pamoja na mkuu wa kitengo hichi cha NSS. Nikahitasha kikao cha siri na cha dharura na wakuu wote wa vitengo vya usalama na wote nikawapa muda wa kukutana majira ya saa nane usiku, hata wote walio kuwa mikoani wote nikawahitaji wafike kabla ya kikao kuanza.

“Muheshimiwa raisi ni kwa nini tusimtangaze makamu wa raisi kama muhalifu hatari anaye tafutwa na serikali?”

Judy aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.

“Mambo hayaendi hivyo kwa watu kama makamu wa raisi”

“Una maanisha nini?”

“Judy ni mara ngapi nina kuambia kwamba makaku wa raisi ni mtu hatari. Mtu mwenye watu wake kile kona. Kinacho paswa ni wewe kuhakikisha kwamba tuna msambaratisha na sio kumtangaza. Si amekimbia mafichoni basi tuta muua huko huko mafichoni na dunia haito kuja kuona jeneza lake wala kaburi lake.”

Judy akanitazama kwa macho ya mshango.

“Kuna oparesheni za kuzungumza na kuna oparesheni za kimya kimya. Wewe ni mwanajeshi amka Judy”

“Sawa mkuu”

Moja kwa moja nikaelekea ninapo ishi.

“Wata kuwa wamekwenda wapi?”

Maria aliniuliza mara baada ya sisi sote kukaa mezani kwa ajili ya kupata chakula cha usiku.

“Nani?”

Nilimuuliza Maria.

“Mama na makamu wa raisi?”

“Bado tuna endelea kufanya upelelezi. Kwa sasa nina kuhitaji utulie na mambo yakienda vizuri nita kujulisha. Ume nielewa”

“Sawa Eddy”

Tukapata chakula hichi kilicho andaliwa na Cauther kisha Maria akaelekea chumbani kwake kulala huku mimi na mke wangu tukibaki sebleni.

“Nadia sijamuona?”

“Alikwenda nyumbani”

“Ahaaa”

*******************************************************************

Ili uwe wa kwanza kupata episode za mbele za hadithi hii kabambe ya X unacho paswa kufanya ni kuwasiliana nami whatsapp 0742334453 au 0657072588. Kama upo Facebook uta ipata kupitia facebook inbox kwenye page yangu ya Story Za Eddy-tz .EPISODE MOJA NI SH 250/= TU. Wahi sasa

*********************************************************************

“Ila binti wa watu nina muonea huruma. Kipindi hichi ni kigumua sana kwake”

“Yaa sikia tu mke wangu kupoteza mzazi ina uma sana”

“Aisee ni kweli mume wangu.”

“Kuna wakati huwa ana zungumza vitu ambavyo hadi nina muonea huruma. Ila ndio hivyo”

“Sasa ina kuwaje kwa makamu wa raisi na mama yake huyu. Muta wapeleka mahakamani?”

“Do!! walisha toroka na kua watu wengi sana katika kitengo cha upelelezi”

“Weee kumbe ni machui wenye ngozi ya kondoo?”

“Ndio hivyo mke wangu”

“Mmmm sasa ina kuwaje?”

“Tuta wapata tu. Labda mimi nisiwe Eddy”

“Mungu akutangulie mume wangu”

“Sawa, nina kikao saa nane usiku”

“Hapa hapa ikulu au nje ya ikukulu?”

“Hapa hapa ikulu”

“Sawa mume wangu”

Tukazungumza mambo mengi hususani na maisha ya mtoto wetu mpya ambaye ata kuja baada ya miezi minne mbeleni. Majira ya saa tano nikamuingiza Cauther chumbani kulala, kwani tayari alisha anza kusinzia sebleni. Nikamlaza kitandani taratibu na nikamshushia neti.

“Usiku mwema mke wangu”

Nilizugumza huku nikimbusu Cauther katika paji la uso wake pamoja na lispi zake kisha nikashuka kitandani. Nikavua suti hii na kuingia bafuni, nikaoga haraka haraka huku nikimfikiria makamu wa raisi majanga aliyo yafanya. Nikafikiria jinsi alivyo nieleza kuhusiana na mama yangu. Nikatoka bafuni, nikachagua suti nyingine, nikaiandaa na kuiweka tayari kwa kuvaa.

‘Je niendelee kuongoza hichi kiti, ili nipambane na hawa washenzi?’

Nilijiuliza huku nikimtazama Cauther namna alivyo lala kitandani.

‘Siwezi kuvunja katiba ya nchi yangu. Nahitaji kuitunza familia yangu. Maisha yangu yote nilikuwa ni mtu wa kutumika serikalini. Sasa ni wakati wa kuyamalizia maisha yangu na familia yangu’

Nilizungumza kimoyo moyo. Nikajifunga taulo kiunoni na nikatoka ndani haa. Nikaingia jikoni nikatafuta kahawa na nikaanza kuitengeneza.

“Bado hujalala”

Sauti ya Maria ikanistua sana kwa maana sikutarajia kumuona jikoni hapa. Nikamtazama jinsi alivyo simama mlangoni mwa jiko hili huku akiwa amevalia nguo ya kulalia nyepesi huku ikonyesha maungo yake ya ndani vizuri.

“Yaaa mbona upo hapa?”

“Nime kosa usingizi chumbani kwangu. Nimeona nije kuchukua japo tunda kwenye friji nitafune tafune kichwa changu kina mawazo sana”

Maria alizungumza huku akipiga hatua za kuingia ndani hapa, bila ya hofu yoyote kwani nina ona chupi nyeupe aliyo ivaa huku maziwa yeke yakiwa yana onekana vizuri kwenye kinguo hichi.

“Sawa”

Maria akafungua friji hii kubwa, akatazama tazama kisha akachukua ndizi.

“Huna usingizi nini kwa maana kunywa kahawa saa sita hii si kujitakia mkesha wa bure bure”

“Yaa nina taka kukesha leo”

Maria akaimenya ndizi hiyo na akaanza kuinyonya mithili ya mwanamke anaye nyona jogoo. Kitendo hichi kikamfanya jogoo wangu kukurupuka ndani ya taulo hili na kuanza kujichora juu ya taulo hili.

“Kwa nini ulioa mwarabu?”

Swali la Maria likanifanya nikae kimya kwa dakika kadhaa.

“Ndio mwanamke niliye mpenda”

“Waswahili wezako huja wapenda?”

“Hata yeye ni mswahili ila utofauti ni rangi ila amezaliwa Tanzania na ana zungumza kiswahili vizuri na niraia wa Tanzania.

“Sawa”

Maria akanisogelea karibu yangu, akanitazama kuanzia usoni hadi eneo la jogoo wangu.

“Ana onekana ana faidi”

Maria alizungumza huku akitaka kunishika jogoo wangu ila nikamuwahi mkono wake na kuudaka.

“Una taka kufanya nini?”

“Nataka mbo** yako”

“Maria tambua wewe ni mdogo wangu na uta baki kuwa hivyo?”

“Mimi na wewe ni tumbo moja kwani. Isitoshe mimi ni mtu mzima nina jitambua na nina maamuzi yangu. Hivyo udada wetu usitufanye ukashindwa kunihudumia”

“Hapana Maria haiwezekani, nina muheshimu sana baba yako na tambu leo ndio tume toka kumpumzisha. Hembu tumuache basi apumzike kwa amani”

Maria akanitazama kwa macho malagevu huku akinisogelea zaidi.

“Hivi una umri gani?”

“Miaka ishirini na nne”

“Bado mdogo sana kwangu”

“Sijali hilo, nahitaji unitomb*** Eddy. Nikiwa katika huzuni huwa nina hitaji mwanaume anitomb** hadi akili yangu iweze kukaa vizuri. Tafadhali Eddy”

Maria akazisogeza lipsi zake karibu kabisa na mimi, akachuchumalia kwani mimi ni mrefu kuliko yeye. Akazigusisha lipsi zake na zangu.

“Hii sio sehemu sahihi, tangulia chumbani kwako nina kuja”

“Huwezi kuja, nina kushika mkono twende wote”

Nikamtazama Maria, kisha nikazima jiko hili linalo endelea kuchemsha kahawa hii. Tukatoka ndani hapa na kuingia ndani kwake. Akafunga mlango kwa ndani, Maria akalifungua taulo langu na taratibu akachuchumaa chini, akamshika jogoo wangu na kuanza kujipiga piga naye mashavuni mwake. Akaanza kumnyonya taratibu huku akiyachezea chezea makend** yangu.

“Mmmm”

Nilitoa miguno ya kimahaba huku nikisikilizia utundu wa binti huyu. Akasimama kisha taratibu tukaanza kunyonyana denda. Nikamvua kinguo chake hichi pamoja na chupi yake. Nikamshika kitumbua chake na kukuta kikiwa kimesha lowana vya kutosha. Nikamlaza kitandani na mtanange huu ukaanza kimya kimya. Kadri muda unavyo zidi kwenda ndivyo jinsi Maria alivyo zidisha vilio vya mahaba hadi ikafikiwa wakati nikamziba mdomo wake. Nikampeleleka moto wa kutosha Maria hadi akaanza kuomba nipunguze kasi kwani nina weza kumua.

“Siwezi kukukoj**a pasipo kwenda kasi, vumilia mpenzi”

Nilimnong’oneza Maria.

“Pumzi ime kwisha baby”

“Lala kifudi fudi basi”

Maria akageuka taratibu huku akionekana kuchoka. Akalala kifudi fudi nikaibana miguu yake na nikaanza kumpelekea moto hadi nikaanza kuwasikia waarabu weupe wakijianda kutoka. Nikamchomoa kwa haraka jogoo wangu na waarabu wote wepupe nikawamwaga juu ya makalio ya Maria.

“Asante Eddy, kweli ume nikata kiu yangu”

“Nashukuru nawe pia. Ila sihitaji mtu yoyote ajue hili?”

“Ni mimi na wewe hakuna atakeya jua”

“Sawa”

Nikashuka kitandani hapa, nikatazama saa ya ukutani na ina onyesha ni saa saba na dakika mbili. Nikajifunga taulo langu.

“Mmm siamki yaani hapana ume nifanya kitu sicho Eddy”

“Poa asubuhi tuta onana, ila hizo shahaw** zifute”

Maria akachukua shuka lilipo kitandani na kujifuta waarabu weupe wote.

“Kiss basi mpenzi”

Nikampiga busu la mdomoni kisha nikatoka ndani hapa pasipo mtu kuniona. Nikaingia jikoni, nikaipasha tena tena kahawa yangu kisha nikajitengea kwenye kikombe na kuanza kunywa taratibu, huku nikirudi chumbani kwangu. Nikamkata Cauther akiendelea kuuchapa usingizi.

‘Samahani mke wangu, mumeo majaribu kama haya huwa ni ngumu sana kuyaruka’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikiweka kikombe hichi cha kahawa juu ya meza, nikaingia bafuni, nikaoga kwa mara ya pili kisha nikajianda kwa ajili ya kikao. Nikaimalizia kahawa yangu na nikatoka ndani hapa. Saa nane kamili nikaingia katika ukumbi wa mkutano ambao vikao vyote vya siri huendeshwa ndani ya ukumbi huu. Watu wote kumi na mbili wakasimama kama heshima. Mara baada ya mimi kukaa nao wakaka. Nikawasalimia wote kwa maana ndani hapa ni mimi na Judy ndio wadogo kiumri.

“Nchi imeyumba kwenye swala zima la ulinzi. Vitengo vingi vya ulinzi NSS na Polisi muna yumba. Kuna matukio ambayo NSS au Polisi mulipaswa kuyashuhulikia kwa uharaka ila munasubiria jeshi ndio liweze kufanya shuhuli hizo. Jambo ambalo ni baya sana ndani ya nchi. NSS ime vamiwa na vijana zaidi ya hamsini wame uwawa. Ikiwa nyinyi ndio kitengo nyeti katika nchi hii kupata habari zote za upelelezi ila mumepigwa na watu wachache sana. Swali langu hapa ni kwamba muna wasaliti ndani yenu au ni munafanya kazi kwa mazoea”

Nilizungumza kwa msisitizo huku nikiwatazama watu wote humu ndani. Kila kmtu akakaa kimya kunisikiliza.

“Kuanzia leo nina kifunga rasmi kitengo cha NSS”

Watu wote wakastuka kwa maana kufungwa kwa NSS ni hatari sana kwenye taifa kwani ndio kitego cha upelelezi na ni kitengo cha siri ambacho kina shuhulika na maswala yote ya upelelezi wa ndani na nje ya nchi ya Tanzania.



Mkuu wa kitengo cha upelelezi kwenye jeshi la polisi akanyoosha mkono na nikampa nafasi ya kuzungumza.

“Muheshimiwa raisi, kitengo cha NSS kimekuwa ni kitengo nyeti sana kwenye hili taifa na ndio muhimili wa hili taifa kwenye maswala ya usalama. Na kitengo hichi kimeanzishwa miaka ya toka stini huko. Sasa ina kuwaje hapo muheshimiwa raisi endapo uta kivunja?”

“Tatizo hujanisikiliza hadi mwisho nina hitaji kuzungumza nini?”

Nikakaa kimya kisha nikaendelea kuzungumza.

“Ipo hivi, NSS imekuwa ni moja ya kitengo ambavyo kwa kipindi cha miaka minne toka kikundi cha X kipotee, imeifanya nchi kuingia kwenye misuko suko mingi sana na matukio makubwa ambayo kusema kweli nchi kama nchi ni lazima tukae na tujitafakari upya. Raisi alitekwa yeye, watu wake na ndege yake. NSS walikuwepo na aliye tekeleza jukumu hilo ni miongoni mwa wafanyakazi hao hao wa NSS. Uwanja wa ndege hadi una tekwa NSS mulikuwepo, kitu ambacho ni kosa kwa kitengo kama chenu kusubiria tukio litokee ndio muzinduke. Kazi yenu nyinyi ni upelelezi na muna paswa kuzuia tukio likiwa tu katika mipango ya kupangwa na kabala halijakamilka na kuleta madhara ila muna subiri tukio litokee ndio tuna pambana na hali ya tukio. Tulipo kuwa Ujerumani, washauri wa raisi walitekwa na vijana ho hao wa NSS. Baadhi yenu hamjui na kama hamjui basi nina wajuza leo. NSS hao hao wamehusika kumtorosha makamu wa raisi na kimada wake wakiwa wana hojiwa ndani ya jengo lao hilo hilo”

“Je muhitaji tuendelee kuwa na nchi yenye kitengo kilicho jaa wasaliti na watu wasio na uzalendo na nchi yao na majukumu yao kwa maana. Wale walio mtorosha makamu wa raisi sio watu kutoka nje. Haiwezekani mtu kutoka nje ambaye hajui kitego kile aingine na avamie na aharibu miundo mbinu kwa kuweka mabomu na kuua watu. Yaani kwa akili ya kawaida tu hata mtu huja soma huwezi amini tena juu ya uwezo wa kitengo kama hicho. Je munahitaji kuendelea na kitengo cha NSS tushuhudie upuuzi unao endelea kila mara?”

Watu wote wakatazamana. Mkuu wa kitengo cha NSS madame Caro akanyoosha kidole.

“Ndio”

“Muheshimiwa raisi kwanza nitangulize kuomba msamaha kwa kila jambo lililo tokea likiwa chini ya ungozi wangu. Nimefanya kazi kwenye kitengo cha NSS huu sasa ni mwaka wa isihirini na tano. Kwenye hii miaka minne iliyo pita hadi kufika leo nikiri kwamba ndani ya kitengo cha NSS kuliingia siasa. Siasa ambayo ilipekea mgawanyiko wa pande mbili upande wa raisi aliye pita na upande wa makamu wa raisi aliye pita kitu ambacho kilikuwa ni kibaya kuliko vitu vyote. Kwa mara kadha niliweza kukaa na raisi aliye pita pamoja na makamu wake na kuwaeleza juu ya hili jambo ila hapakuwa na aliye nipa jibu sahihi kwani walikuwa juu yangu na cheo kikubwa dhidi yangu.”

“Madam Caro kabla hujaendelea, una muda gani toka uwe kiongozi wa NSS”

“Huu sasa ni mwaka wa tisa mkuu”

“Okay endelea”

“Nilikuja kumkazania sana raisi kutoa huu mgawanyiko kwenye kitengo nyeti kama NSS ila raisi akaonekana kuto kuwa na kauli. Ndipo nilipo kuja kugundua kwamba makamu wa raisi ana nguvu kubwa kuliko raisi. Na makamu wa raisi ndio msemaji wa mwisho kwenye nchi kuliko raisi. Mara kwa mara tuliletewa majina ya wafanyakazi wapya wa kitengo cha NSS kutoka chuoni na sehemu vitego vingine vya jeshi kama polisi na jeshini. Watu hao ndio nilikuja kugundua kwamba wapo sambamba na makamu wa raisi japo walikuwa wana kuja kwa tiketi ya ofisi ya raisi na si ya makamu wa raisi. Ndani ya kipindi hicho cha miaka mine muheshimiwa raisi nilikuwa nina fanya kazi nje ya weledi wangu na nilipokuwa nina hoji nilikuwa nina nyamazishwa kinywa changu na nilipo kuwa nina chukua hatua basi basi hatua hizo zilikuwa zina wekewa vizingiti au kutolewa amri na zina yayuka na hakuna kinacho endelea na ilifikia hatua nikawa nina tumiwa vitisho kwamba ninavyo endelea kusimama kidedea basi ita pelekea familia yangu kuuwawa na nikiwa kama mama mwenye uchungu wa wanangu sikuhitaji kuona hilo jambo linatokea ndio maana nilikuwa kimya muheshimiwa raisi”

Maneno ya madame Caro yakanifanya nishushe pumzi taratibu.

“Nina imani hata nyinyi huko mulikuwa muna kutana na changamoto kama hizi?”

“Ndio muheshimiwa raisi”

Karibia watu wote walijibu, nikawatazama na kwa kweli sina wa kumlamu kwani hata mimi mwenyewe niliingizwa kwenye jeshi na makamu wa raisi hivyo kama ninge kuwa na akili mbovu basi leo hii ninge kuwa upande wake na ninge fanya mambo ya kila aina kama jinsi anavyo hitaji yeye.

“Tumeanguka na tayari tumesha toka kwenye utawala wa kuwasujudia watu. Hili ni taifa la demokrasia na sio taifa la kifalme kwamba mfalme akipita ni lazima tumpigie magoti na kumsujudia. Wote mumeona alicho kifanya makamu wa raisi. Kama wewe ni mtu wa makamu wa raisi nyoosha mkono juu”

Watu wote wakatazamana huku wakiwa kimya. Nikasubiri kwa dakika moja nzina na hapakuwa na aliye nyoosha mkono.

“Ina maana sisi wote ni kundi moja si ndio?”

“Ndio muheshimiwa raisi”

“Nina hitaji kila mmoja kwenye kitengo chake. Jeshini, polisi, NSS wenyewe kila mmoja atoa vijana elfu moja. Shupavu, wazelendo na wenye mapenzi na nchi yao. Vijana wenye uwezo wa kukubaliana na hali yoyote ndani ya nchi yao. Nahitaji vijana hao waunde kitengo kingine kipya. Kitengo cha watu hatari, watapatia mafunzo kama niliyo pitia mimi, mafunzo ya kuwafanya wawe ni watu hatari na mafunzo ambayo hayapo jeshi la polisi, wala jeshi la kawaida wala eneo NSS wenyewe. Vijana hao kwa ujumla wata unda kitengo kipya kabisa cha X”

Nikaona sura za watu zikiwa zimeanza kutawaliwa na matabasamu, wakanipigia makofi ya furaha.

“Kikundi cha X labda niwaeleze sifa zake mujue. Hawato kuwa watu wa kawaida, hawato kuwa watu wenye majengo yanayo onekana kama NSS, ofisi zao zitakuwa ni tofauti na tulivyo zoea. Ukutanaji wao uta kuwa ni wa code na sio wa kuitana ofisini. Utendaji wao wa kazi uta kuwa ni mgumu kuliko watu wengine na hakuna mtu yoyote tofauti na walimu wao watako kuwa wana jua hao jamaa ni wafanyakazi wa X.”

“Hapo muheshimiwa raisi ume nena”

Madam Caro alizungumza huku akiwa amejawa na tabasamu.

“Endapo ikataokea X mmoja akasaliti aka fanya maasi kinyume na taratibu na nchi. Adhabu yake ni kifo yeye na kizazi cheke chote.”

Nikaona nyuso za watu zinavyo jawa na mshangao ambao hawajautegemea.

“Hawato hojiwa na chombo chochote cha habari. Hawato onekana kwenye chombo chochote cha habari na hawato kuwa na utambulisho mmoja wala wa sura moja. Hivyo basi ni kwenda kuunda kikosi kikubwa cha watu ambao hata shetani mwenyewe ata nyoosha mikono juu”

“Hahaaahahaa”

*******************************************************************

Ili uwe wa kwanza kupata episode za mbele za hadithi hii kabambe ya X unacho paswa kufanya ni kuwasiliana nami whatsapp 0742334453 au 0657072588. Kama upo Facebook uta ipata kupitia facebook inbox kwenye page yangu ya Story Za Eddy-tz .EPISODE MOJA NI SH 250/= TU. Wahi sasa

*********************************************************************

Watu wakacheka kidogo.

“Nakaribisha maswali”

“Ahaa mkuu endapo tuta kuwa na watu elfu tatu au nne, huoni itakuwa ni idadi ndogo sana ya wapelelezi wa nchi, ukiachilia na idadi iliyopo sasa hivi?”

“Ni heri kuwa na marafiki wawili wa ukweli na wanao kuunga mkono kwenye hali yoyote. Ngumu au mbaya kuliko kuwa na marafiki elfu moja ambao ni wanafki. Sisi tulikuwa wanne tu, ila mziki wetu wote muliusikia na hakuna hata mmoja aliye tujua kati yenu zaidi ya raisi na makamu wa raisi. Je wakiwa vijana elfu nne kuta kuwa na nini? Lazima nchi inyooke na kwenye hichi kikosi cha sasa nita hitaji wanawake si chini ya elfu mbili na mia tano. Wazuri wenye mvuto na wenye uwezo wa kumshawishi gaidi akawa askofu”

“Hahaaaa”

“Sasa muheshimiwa raisi hawa vijana wengine ambao wapo kwenye kitengo cha NSS ita kuwaje?”

“Hao walio salia tuta waingiza kwenye vitengo vingine kuchukua nafasi za hawa walio tolewa huku”

“Je mafunzo ya hao ita chukua muda gani?”

“Miaka mitatu”

“Sasa mkuu kwenye miaka mitatu hiyo tuta kosa wapelelezi huoni kama ni hatari?”

“Sijasema nchi isiwe na wapelelezi. Hamjanielewa maana yangu ni kwamba lazima nchi iwe na kikosi cha watu hatari, kikosi cha watu wanao weza kujitolea kufa. Polisi muna wapelelezi, jeshini muna wapelelezi NSS mulikuwepo ila ndio usaliti umejaa ndani yake. Kuondoka NSS ni kuweka uwiano sasa wa vitengo vyote vya ulinzi vianze kufanya kazi kuanzia jeshi na polisi”

“Muheshimiwa raisi samahani kwa kuuliza swali hili. Tuna ona una malengo makubwa na hii nchi ila kumbuka una kipindi cha miezi mitatu tu na siku za miezi mitatu zimesha lika. Je hicho kikosi kitakwenda kufanya kazi pale endapo hauto kuwa madarakani kwa maana ni lazima kitengewe bejeti na raisi akiidhinishe je raisi ajaye ata weza kukubaliana na hili jambo au litafutiliwa mbali na kuzidi kuitia hasara nchi au una mpango wa kugombania uraisi baada yamiezi hii kuisha?”

Nikashusha pumzi kwa manna hili swali ni zuri sana.

“Sina mpango wa kugombania uraisi. Kwanza sihitaji kuvunja katibaya nchi yangu, sasa hivi nina miaka thelathini na tatu. Bado miaka saba niwe na umri wa miaka arobaini ili katiba inikuli kuwa raisi wa nchi hii. Leo mimi nikisimama kuwa raisi ita fikia kipindi wapo watakao taka kuwa maraisi kwa umri wangu na katiba ita watoa na tuta zua uwalakini”

“Ila muheshimiwa raisi una onaje tua badilisha katiba na kushusha umri wa raisi hadi miaka thelathini na tano, ita kuwa ni nafasi nzuri kwa wewe kugombania. Katika vingozi wenye mapenzi na uchungu wa nchi yao niliyo wahi kuwaona hapa Tanzania. Wewe ni mmoja wao na una maono makubwa na hii nchi ina hitaji viongozi kama wewe. Makamu wa raisi ana mtando mkubwa sana ila ukiwepo wewe huto weza kuiangusha nchi uta pambana naye hadi dakika ya mwisho”

“Hapana, ninge penda mumpendekeze mtu wa kisiasa ambaye ata ishi kwenye haya mawazo bila kukwepesha”

“Ila muheshimiwa raisi kama unavyo fahamu hawa viongozi wa kisiana ni mabomu kabisa. Watakujia kwa sura ya furaha ila mwisho wa siku wata ingia kwenye mambo ya kipuuzi wanayo yajua wao”

“Ila mimi nilikuwa nina mfikiria waziri mkuu aliye pita”

Nilipendekeza jina la waziri mkuu.


ITAENDELEA


1 comment:

BLOG