Search This Blog

Wednesday, November 18, 2020

SIN SEASON 2 SEHEMU YA 3/10

   


SIN SEASON 2

WRITER…………………………………………EDDAZARIA G.MSULWA
WEBSITE………………………………………… www.storyzaeddytz.com
CONTACT……………………………………….. 0657072588/0768516188
AGE……………..18+

SEHEMU YA 3 KATI YA 10


“Jose niambie ni nini ulicho kiona”

Josephine akamtazama Magreth kwa sekunde kadhaa huku machozi yakimbubujika usoni mwake.

“Nina kiona kifo chako Mage”

Magreth moyo ukamstuka, akahisi kama moyo ume msimama kwa sekunde kadhaa kwani hakutarajia kusikia taarifa kama hiyo.

“Ume sema?”

“Mungu ame nionyesha kifo chako na hakipo mbali kipi siku hizi za usoni. Nina umia Mage nita baki na nani ikiwa wewe nime kuzoea rafiki yangu”

Magreth hata hakumsikia kabisa Josephine ni kitu gani anacho kizungumza. Akasimama na kuelekea ndani huku akiwa hana hata nguvu za kutembea vizuri. Ikambidi sasa Josephine kumfwata na kumshika mkono kwani ana muona rafiki yake huyo akiyumba huku akiwa amepoteza furaha kabisa.

“Nitatembea”

Magreth alizungumza huku akiuchanisha mkono wake na mkono wa Josephine. Magreth akapitiliza moja kwa moja hadi chumbani kwake na kuufunga mlango wake kwa ndani.

“Mage Mage fungua”

Josephine aliita huku akigonga mlango huo kwa nje.

“Jose kuna nini?”

Juma aliuliza huku akimtazama kwa umakini Josephine aliye jawa na machozi mashavuni mwake. Josephine akashindwa kuvumilia na kujikuta akimkumbatia Juma kwa nguvu, kwa akili ya haraka haraka Juma akahisi labda wasichana hao wame weza kugombana. Taratibu akambeba Josephine na kurudi naye sebleni.

“Mume gombana mke wangu”

Josephine akajibu kwa kutingisha kichwa akiashiria kwamba hawajagombana.

“Sasa mbona mwenzako ame jifungia kwa ndani?”

“Mume wangu nime pewa maono yake ndio yame tuvuruga na kutukosesha amani na furaha”

“Maono gani hayo?”

“Magreth ata kufa baada ya siku tatu”

Juma akastushwa na habari hiyo, macho yakamtoka huku mapigo ya moyo yakianza kumuenda kasi sana. Hata hamu ya kuendelea kumuuliza Josephine maswali ikamuisha, koo lake likahisi kiu kubwa ya maji. Akachukua jagi la maji pamoja na glasi iliyopo mezani na kuanza kumimina kiasi cha maji kwenye glasi hiyo na kuanza kunywa maji hayo huku akiwa haelewi hata afanya nini kwani taarifa hiyo kwa kweli sio nzuri kabisa kwao.

Mage akajitazama kwenye kioo cha dreasing table iliyopo ndani hapo. Uzuri wake, afya yake vyote vina kwenda kuingia ardhini ndani ya siku chache alizo ambiwa na Josephine. Taratibu akafungua droo iliyopo pembeni mwa kitanda chake. Akaichukua bastola yake, akaitazama vizuri, kisha akachomoa magazine ya bastola hiyo na kukuta risasi za kutosha. Akairudisha magazine hiyo kisha akatoka sebleni huku akiwa ameishika bastola hiyo. Jambo hilo lika washangaza sana Juma na Josephine.

“Jose natambua kwamba sinto kufa kwa kuumwa si ndio”

Josephine akamtazama Magreth na akapata kigugumizi cha kuweza kujibu swali hilo na akabaki akimkodolea macho Magreth.

“Nijibu”

“Ndio”

Josephine aliujibu huku macho yake ukitazama mkono wa Josephine ulio shika bastola hiyo.

“Nani ata niua?”

Magreth aliuliza kwa msisitizo na kumfanya Josephine kushusha pumzi nyingi. Juma akaka kimya huku akimtazama bosi wake huyo ambaye ana onekana kuwa hana masihara na maswali anayo muuliza Josephine.

“Jose niambie ni nini unacho taka kufanya?”

“Endapo nita muua ambaye ana hitaji kunia kuniua nina imani kwamba nita kuwa nimejiepusha kutoka kwenye kifo au una semaje Juma?”

“Ahaa….ni kweli mkuu”

Juma alijibu kwa kubabaika kwa maana hataki kumkwaza bosi wake ambaye ana onekana kuchanganyikiwa.

“Mage ume panic kwenye hili swala. Nina kuomba nikae chini nitulie nimuombe Mungu ili niweze kumuomba anipe njia ya kuweza kutuepusha kwenye hivyo vifo”

“Ngoja kwanza una sema vifo una maanisha nini?”

“Mimi na wewe tuna kwenda kufa. Wataanza kukuua wewe kwa maana wewe ndio mtu wa pekee mwenye uwezo wa kunilinda”

Magreth taratibu akajikuta akikaa kwenye sofa la pambeni.

“Ni nani ambaye ana mpango wa kutuua ikiwa hatuja mkosea kitu chochote huyo mtu”

“Ni x-boyfriend wako Evans ndio amewalipa wauaji kwa ajili ya kutuua sisi.”

“Evans huyu ninaye mjua mimi?”

“Ndio huyo, kwa sasa amekuwa ni shetani na sio yule Evans ambaye alikuwa mnyenyekevu mbele yako”

“Shiti sasa tuna fanyaje?”

“Ndio acha nimuombe Mungu anipatie njia. Nina imani ana makusudi sahihi ya kutuonyesha hivi ili tuweze kufahamu ni mambo gani yanayo kuja mbele yetu ili tujue ni jinsi gani ambavyo tuna weza kuepuka au ulitaka itokee kama suprize kwetu?”

Josephine aliuliza kwa msisitizo.

“Hapana”

“Basi acha niweze kuomba”

Magreth akakubaliana na pendekezo la Josephine na akaondoka sebleni hapo na kuwaacha Juma na Magreth wakiwa katika wakati mgumu kimawazo.

“Bosi”

“Mmmm”

“Tuna fanyaje?”

“Juma hapa nilipo nime changanyikiwa, sijui tuna fanya nini?”

“Daaa hilo swala ni gumu una jua?”

“Ndio”

Magreth alijibu kinyonge huku akijilaza kwenye moja ya sofa refu huku akianza kutafakari ni kitu gani ambacho kuna mfanya Evans kuwalipa watu kwa ajili ya kumuua.

***

Raisi Mtenzi akawatazama washauri wake ambao wamekutana naye kwenye kikao hicho cha dharura kabla hata ya kwenda kuzungumza na raisi wa Marekani.

“Muheshimiwa hayo maamuzi ambayo una taka kuyafanya ni maamuzi magumu sana, ambayo yana weza kuifanya nchi kuingia kwenye mambo mengi. Moja wapo ni vita vya wenyewe kwa wenyewe kwa manaa kama munavyo jua jinsi Wamarekani walivyo wachonganishi. Wanaweza kupandikiza hata kundi la kigaini hapa nchini na likaleta shida na wakawawezesha kwenye maswala ya silaha na mbinu za kijeshi”

Mr the Brain alizungumza huku akimtazama raisi Mtenzi usoni mwake.

“Ni kweli muheshimiwa kama unavyo ona. Shambulizi la Al-Shabab jinsi lilivyo leta maafa ambayo kwa kweli yae tupotezea watu muhimu sana na mambo mengi. Hembu tuwache wajenge huu mji alafu mambo mengine yata fwata”

Mzee Mbogo alizugumza kwa sauti ya upole. Raisi Mtenzi akawatazama wazee hao ambao kwa siku kadhaa zilizo pita aliweza kuwapinga maamuzi yao na zawadi aliyo ipata ni kuondokewa na mtu muhimu pamoja na jiji ambalo ndio kitovu cha biashara nchini Tanzania kuparanganyika na kuwa kama magofu ya kihistoria.

“Hivi mume tambua ni kitu gani ambacho Wamarekani wame kijia nchini kwetu?”

Mzee Mbogo na mr the Brain wakatazamana. Kisha kila mmoja akatingisha kichwa akimaanisha kwamba hafahamu.

“Wamarekani wame kuja hapa kwa malengo makuu mawili. Moja ni kutupumbaza ili tuweze kuwaamini kwamba wame kuja kutujengea mji wetu. Lengo la pili ni kuchukua hadhina na yamadini iliyopo katika ardhi ya hapo posta. Hadihina hiyo endapo ita chukuliwa, Wamarekani wata kuwa na nguvu mara dufu na nguvu walizo nazo hivi sasa. Endapo hathina hiyo tuta ipata sisi basi nchi yetu ina kwenda kuwa na nguvu sawa na wao au hata kuwapita. Hembu jiulizeni swala la kujitolea tu ina kuwaje kama ombi lako likikataliwa na una amua kushinikiza kuendelea kujitolea lasivyo una fanya maamuzi ambayo una hisi yana mkandamiza yule unaye msaidia”

Raisi Mtenzi alizungumza kwa sauti ya upole na kuwafanya mzee Mbogo na mr the Brain kushusha pumzi kila mmoja kwa wakati wake.

“Ukiwa na akili timamu ni lazima uta litazama hili jambo kwa jicho la tatu”

“Muheshimiwa wewe ume fahamu vipi kama kuna hadhinakwenye hilo eneo?”

“Kuna binti ame niambia”

“Huyo binti ni nani?”

Mzee Mbogo aliuliza huku akimtazama raisi Mtenzi usoni.

“Huyo msichana ndio aliye weza kuwaonyesha waokoaji eneo ambalo nilikuwa nime fukiwa na kifusi na binti huo ndio ambaye aliweza kutengeneza matangazo kwenye mitandao ya kijamii ya kuwahimiza watu kuondoka jijini Dar es Salaama kwa maana sio salama na nina imani hata nyinyi pia muliondoka kwa kumuamini na kweli kilitokea cha kutokea japo kuwa tulihakikisha kwamba tuna tafuta hayo mabomu ila hatukuweza kupata bomu hata moja”

“Mmmm muheshimiwa sawa una muamini huyo binti. Asije kuiingiza nchi kwenye mahusiano mabaya na mataifa makubwa?”

“Muheshimiwa una onaje uka iona hiyo hadhina kabla ya kufanya hayo maamuzi”

“Ni kweli au unaonekana aka kupeleka wewe mwenyewe kwenda kuona hiyo hadhina kisha ndio uka fanya maamuzi?”

“Nina imani hiyo hadhina sio kitu cha kukaa juu tu ya ardhi, ni kitu cha kuchibwa kwenda chini hivyo mukisema kwamba twende sasa hivi tuta ishia kuona magorofa yaliyo anguka pale”

“Muheshimiwa kwa heshima yako na nafasi uliyo tupatia tena kwa ajili ya kukusaidia katika serikali yako hii. Nina kuomba umpigie simu binti huyo aweze kuja hapa ili sisi watatu tuweze kumuhoji”

Mr the Brain alizungumza kwa kujiamini.

“Ni kweli muheshimiwa hembu fanya hivyo”

Raisi Mtenzi akakubaliana na washauri wake hao ambao kwa sasa ana wasikiliza sana tofauti na pale awali alivyo kuwa kiburi na kuyaamini maamuzi yake. Simu ya Josephine ikaanza kuita na baada ya sekunde kadhaa ikapokelewa.

“Haloo muheshimiwa una zungumza na Magreth”

“Ohoo habari yako Mage”

“Salama tu mkuu.”

“Josephine yupo wapi?”

“Yupo chumbani ana sali muheshimiwa”

“Tafadhali kama ikiwezekana nina kuomba sana uweze kumleta hapa ikulu. Kuna jambo muhimu sana ambalo nina hitaji kuzungumza naye.”

“Ohoo huyu hapa ame toka chumbani”

“Mpatie simu”

“Shikamoo muheshimiwa”

“Maharaba. Tafadhali nina kuomba sana uweze kuja ikulu”

“Sasa hivi!!?”

“Ndio”

“Sawa ngoja nijiandae”

“Rafiki yako ata kusindikiza”

“Sawa muheshimiwa”

Raisi Mtenzi akakata simu na kuwatazama mr the Brain pamoja na mzee Mbogo aliye jawa na hamu ya kumuona msichana huyo kwani ana amini mtu aliye mpatia taarifa juu ya milipuko ni Evans na sio huyo msichana anaye itwa Josephine. Baada ya lisaa moja, Juma, Josephine na Magreth wakafika ikulu hapo. Josephine moja kwa moja akaelekea ofisini kwa raisi Mtenzi. Akasaimiana na wazee hao kisha akaketi kwenye moja ya sofa.

“Huyu ana itwa Josephine. Josephine, huyu ana itwa mr the Brain ni mshauri wangu kwenye maswala ya kijamii, kisiasa, afya na kadhalika. Huyu ana itwa mzee Mbogo ni mshauri wangu katika maswala ya usalama wa taifa kwa ujumla.”

“Nina washukuru kuwafahamu”

“Nasi pia tuna shukuru”

“Tume sema pamoja”

Mr the Brain alizungumza huku akianza kucheka.

“Lengo ambalo tume kuitia hapa, washauri wangu wana hitaji kuhakikishiwa kwamba hiyo hadhina ipo au haipo ili kama ni kufanya maamuzi na serikali ya Marekani basi isije ikatokea malalamiko ya kwamba tume fanya maamuzi magumu ikiwa hadhina tuliyo itarajia”

Josephine akashusha pumzi huku akimtazama raisi Jery pamoja na wazee hao wawili.

“Hadhina ipo tena ni nyingi sana.”

“Binti je una weza kumpeleka muheshimiwa hapa au tuka enda wote kwenda kuiona”

“Sio rahisi kwenda na kuiona”

“Una maanisha nini?”

Mr the Brain aliuliza huku akimkazia macho Josephine.

“Hadhina hiyo ipo chini ya ardhi tena kwenye mapango ambayo ni hatari na pasipo damu ya mtu mmoja tu duniani kupatikana basi hayaweze kufunguka na wala njia ya kuelekea kwenye mapango hayo haito weza kufunguka.”

Kauli ya Josephine ikamfanya raisi Mtenzi kukaa vizuri kwenye kiti chake kwani ugumu wa jambo hilo ana anza kuuona mapema sana.

“Ni damu ya nani huyo na huyo mtu ana patikana wapi?”

Mzee Mbogo aliuliza huku akiwa na shahuku ya kuhitaji kufahamu.

“Ni mimi. Damu yangu ndio ina uwezo wa kufungua njia ya kueleaka kwenye mapango hayo na mlango wa kuingilia kwenye mapango hayo.”

“Basi kumbe upo, una weza kutupeleka tukaona au una semajae muheshimiwa raisi?”

Mrs the Brain alizungumza huku akiwa na shahuku kubwa iliyo changanyikana na furaha.

“Ni kweli Josephine tupeleke ili tukaone hiyo hadhina na kama tuta fanya maamuzi ya kuwakatalia Wamarekani katika ujenzi wao basi niwakatalie nikiwa na uhakika.”

“Muheshimiwa raisi nina kuomba uweze kuniamini. Hadhina ipo, fanya maamuzi ya kuwaondoa kwanza Wamarekani kwa maana hapa tulipo tu wana tusikiliza na kila jambo ulilo zungumza ndani ya ofisi yako wanalo na endapo tukaenda sasa hivi basi watatufwata nyuma na hawato ona hasara ya kutuua tukiwa ndani ya mapango hayo na ikawa njia rahisi ya wao kuchukua hadhina hiyo yote”

Maneno ya Josephine yaka wastua sana raisi Mtenzi na washauri wake kiasi cha kuwafanya waanze kutazamana huku raisi Mtenzi akiwahisi washauri wake hao mmoja wapo ata kuwa ni msaliti na ana fanya kazi na Wamarekani.



“Ni nani mwenye kifaa cha kurekodi sauti?”

Raisi Mtenzi alizungumza huku akiwatazama mzee Mbogo na mr the Brain.

“Sio wao”

Josephine alisimama na kusogelea moja ya ua pambo lililopo ofisini hapo. Akalichunguza kwa sekunde kadhaa kisha akatoa moja ya jani ambalo kwa mtazama wa kawaida una weza kuliona ni jani ila lime tengenezwa kitaalamu na lime wekewa vinasa sauti ambavyo kila kitu kinacho endelea ndani ya ofisi ya raisi kina sikika. Raisi Mtenzi, mzee Mbogo na mr the Brain wote wakajawa na mshangao. Josephine akaweka kidole kimoja mdomoni mwake akiashiria kwamba wasizungumze chochote. Josephine akawaomba raisi Mtenzi na washauri wake kutoka ndani hapo na wakatii huku wakiliacha uwa hilo ndani ya ofisi hiyo.

“Lile ndio ua linalo rekodi mazungumzo na yana wafikia wanajeshi wa Marekani”

“Ni nani aliye liweka?”

Raisi Mtenzi aliuliza ila akakosa jibu hili kwa maana ofisi yake kipindi alipo kuwa ana umwa ilikuwa chini ya makamu wake wa raisi ambaye kwa sasa ni marehemu.

“Muheshimiwa ina bidi kufanya jambo juu ya hili swala kwa maana Wamarekani walipo fikia hapa ni pabaya sana"

Mr the Brain alizungumza na kumfanya raisi Mtenzi kutafakari kwa sekunde kadhaa.

“Nina mpigia balozi wao kuja hapa”

“Hiyo haito kuwa solution muheshimiwa.”

Mzee Mbogo alishauri.

“Sasa tufanyaje?”

“Jambo la kufanya hapa muheshimiwa ni kujaribu kutengeneza mtego wa kuwakamata hao wana tufwatilia kwa maana tuna weza kuhisi Wamarekani kumbe ndani yake kuta kuwa na watu wenye lengo la kutupeleleza”

“Sasa mpango gani tufanye?”

“Muheshimiwa, kama hoto jali nina kuomba hili swala tumshirikishe rafiki yangu Magreth”

“Kwa nini Magreth?”

“Moja ni professional kwenye mambo ya upiganaji ana uwezo mkubwa na huyo ndio mtu wa pekee aliye weza kupambana na wanajeshi wako pamoja na walinzi wako wambao wame pata mafunzo ya hali ya juu ila akafanikiwa kuwamudu na kukutoa pale Muhimbili”

Josephine alimpigia debe rafiki yake huyo ili mradi kuhakikisha kwamba hamuachi Magreth kwenye kila eneo ambalo ana kuwepo yeye.

“Wageni walio ambatana na huyu binti wapo wapi?”

Raisi Mtenzi alimuuliza mmoja wa walinzi wake.

“Wapo chumba cha kupumzikia”

“Muite Magreth”

“Sawa mkuu”

Mlinzi huyo akaondoka na kuwaacha raisi Mtenzi na washauri wake nje ya ofisi yake.

“Kuna clip ambayo ulitolewa pale hospitalini muheshimiwa. Una taka kuniambia kwamba binti huyo ndio aliye fanya mambo hayo yote?”

Mzee Mbogo alizungumza huku akimtazam Josephine usoni mwake.

“Hembu niione hiyo clip”

Mzee Mbogo akaiweka clip hiyo kwenye simu yake na kumuonyesha raisi Mtenzi. Raisi Mtenzi akamshuhudia jinsi Magreth aliye valia nguo za kinesi, akipambana na wanajeshi pamoja na walinzi wake.

“Ndio huyo ni Magreth”

Josephine alizungumza huku naye akiitazama clip hiyo ya video kwa maana yupo karibu na raisi Mtenzi. Magreth akafika eneo hilo huku akiwa ameongozana na mlinzi huyo aliye agizwa kwenda kumchukua.

“Mage una fahamu hii”

Raisi Mtenzi alizungumza huku akimkabidhi Magreth simu hiyo. Magreth akastuka kidogo mara baada ya kuona hivyo clip kwa maana anyae onekana hapo ni yeye pamoja na Juma ambaye yeye hakuwa mpambanaji. Magreth akamtazama Josephine na kumumkuta akiwa amejawa na tabasamu pana sana usoni mwake ambalo kidogo likamtoa wasiwasi.

“Ndio muheshimiwa ni mimi”

“Nime lindwa na walinzi wengi sana ila sijawahi kumuona mwenye uwezo wa kupambana kama uwezo wako”

“Nina shukuru muheshimiwa”

“Sasa acha niende kwenye poiti tuliyo kuitia hapa. Wamarekani katika moja ya ua la pambo katik ofisi yanug wame weza kutehe kinasa sauti ambacho kila tulicho kizungumza ndani hapo waa kisikia. Sasa tuna hitaji kutengeneza mtego wa kuwafanya waweze kuingia kwenye kumi na nane zetu ili hata baadae mahusiano yetu na wao yana kwenda kuharibika basi tuweze kuwa na kidhibitisho kwamba chanzo kikuwa ni wao kutupeleleza kwa kutege kinasa sauti ndani ya ofisi ya raisi”

“Sawa muheshimiwa raisi nimekuelewa. Je ungependa tutengeneze mtego gani?”

“Kwa ujuzi wangu. Wamarekani ni watu wajanja sana muheshimiwa raisi, ninacho kiona ni tutumie nafasi ya huyu binti kukubali kutupeleka kwenye hilo eneo ambalo kuna hadhina kisha huyu msichana aweze kutupatia back up.”

Mr the Brain alizungumza na kuwafanya watu wotte kumtazama raisi Mtenzo.

“Hilo wazo ni zuri sana, ila lina uhatari ndani yake”

“Ni kweli muheshimiwa ila hatuna jinsi. Huyu msichana si yupo vizuri kwenye mambo ya kupambana”

“Ndio”

Muheshimiwa nita kwenda na huyu Josephine ila nita ondoka hapa na msafara wako alafu huyu Magreth ata tupatia back up”

“Josephine una weza kulifanya hili?”

“Ndio muheshimiwa”

“Magreth?”

“Ndio ila nina omba niweze kurudi nyumbani nikachukua vifaa vyangu ili niweze kuifanya hiyo kazi”

“Sawa una dakika hamsini”

“Nashukuru muheshimiwa”

Magreth akaelekea alipo Juma na wakaondoka wote na kuanza kurudi nyumbani.

“Mkuu mbona kama una wasiwasi?”

Juma alimuuliza Magreth huku akimtazama jinsi alivyo jawa na mawazo.

“Kuna kazi moja ya hatari nime pewa kuifanya hiyo kidogo ina nipa wasiwasi”

“Kazi gani?”

“Wamarekani wana ihitaji ile hadhina ambayo Josephine ana waambia. Sasa wame tega kinasa sauti ofisi kwa raisi hivyo mipango na kila kitu cha raisi kina sikika upande wa pili wa Wamarekani. Hivyo tuna hitaji kuwakamata wahusika na mimi ndio nime wepa jukumu hilo”

“Mmmm mkuu mbona kama hilo jambo ni zito sana?”

“Ni kweli ni zito ila ndio hivyo nita fanyaje best”

“Sasa mkuu kumbuka kitu alicho kizungumza Josephine kuhusiana na maono yake. Isije hii ikawa ndio safari”

Juma alizungumza kwa sauti ya upole na kuzidi kumtia wasiwasi Josephine, hata kama ni jasiri kiasi gani ila linapo kuja swala la kufa na una tambua kwamba una siku chache za kuishi duniani basi hata ujasiri huwa una potea kabisa. Magreth akashusha pumzi nyingi kwa maana hatambui ni kitu gani kina kwenda kutokea katika kazi hiyo. Wakafika nyumbani na Magreth akaanza kujiandaa haraka haraka. Alipo hakikisha kwamba yupo tayari, akatoka chumbani kwake huku akiwa amebaba begi la mgoni pamoja na upanga mrefu ambao ana utumia.

“Uta linda nyumba sawa Juma”

Magreth alizungumza huku funguo yake ya pikipiki ikia mkononi mwake.”

“Sawa ila kuwa makini sana bosi. Tambua kuna watu nyuma tuna kutegemea”

Juma alizungumza kwa sauti ya upole huku akimtazama Magreth usoni mwake.

“Usijali, niombee nirudi salama”

“Sawa nakuombea”

“Hakikisha umfungulii mtu yoyote geti hadi upate udhibitisho kama ni sisi”

“Sawa mkuu usijali katika hilo”

“Haya”

Wakatoka nje, Magreth akapanda pikipiki yake huku akimtazama Juma aliye simama getini huku akimsubiri bosi wake huyo atoke ili afunge geti. Magreth akavaa helment ngumu ya pikipiki hiyo kisha akaondoka eneo hilo. Akafika kwenye moja ya sheli na kujaza mafunta tenki nzima ya pikipiki hiyo na kuelekea ikulu. Kutokana ana kitambulisho na raisi ame amua kumpitisha kama mtendaji wake wa serikali akaruhusiwa kuingia na silaha zake.

“Hei ume rudi”

Josephine alizungumza huku akiwa na furaha moyoni mwake.

“Yaa ni nini kinacho endelea hapa”

Josephine akafungua moja ya ofisi na kumuona mzee Mbogo akifanyiwa makeup iliyo mpelekea kufanana na raisi Mtenzi.

“Kwa nini ana fanyiwa makeup”

Magreth alumuuliza Josephine huku akifunga mlango wa chumba hicho.

“Raisi hawezi kwenda kwenye hilo eneo, ndio maana huyu mzee ana pigwa makeup itakayo mfananisha na raisi Mtenzi”

“Ila Josephine niambie kitu kimoja nielewe”

“Niambie”

“Nita kufa kwenye hii kazi au?”

Josephine akashusha pumzi huku akimtazama Magreth usoni mwake ambaye ana onekana kujana na woga.

“Huwezi kufa, nina muomba Mungu aweze kutuepushia kifo sisi sote”

“Mwenzi kusema kweli nina ogopa kuifanya kila kitu. Yaani nina fanya kwa sababu ya heshima yangu kwa raisi. Ila ingekuwa sio hivyo sasa hivi ninge kuwa nipo nyumbani nime lala”

“Usijali nime muomba Mungu juu ya hili na nina imani kwamba ata jibu maombi yetu”

“Raisi ana wahitaji”

Mlinzi wa raisi Mtenzi alizungumza na wakaanza kumfwata na kuingia ofisini kwake. Wakawakuta walitaalamu wa mambo ya maswaliano wakiwa wamesha andaa kila kinasa sauti kwa ajili ya kazi hiyo.

“Hivi ni vinasa sauti ambavyo muna kuwa muna vitumia kuwasiliana na sisi”

Jamaa mmoja alizungumza huku akiwakabidhi Josephine na Magreth vinasa sauti hivyo vidogo vya kuvaa masikioni.

“Mage hilo panga ni la nini?”

Raisi Mtenzi aliuliza huku akiwa amejawa na mshangao usoni mwake.

“Ni kwa ajili ya kujilinda muheshimiwa”

“Sawa muwe makini”

“Tuna shukuru muheshimiwa raisi. Hicho kinasa sauti chao kipo wapi?”

Kijama mmoja akamuonyesha Magreth jani la ua hilo la plastiki(urembo) jinsi lilvyo tengenezwa vizuri.

“Kwa hiyo hapa wana tusikia?”

“Hapana tukizima hichi kikata sauti chetu basi hawato weza kutusikia”

“Zimeni alafu raisi na Josephine muzungumze kwamba muna kwenda”

“Tumesha fanya hivyo”

Raisi Mtenzi alijibu.

“Ahaa sawa. Eneo ni wapi?”

Magreth aliuliza huku akimtazama raisi Mtenzi usoni mwake.

“Ni hapo Posta kwenye zile gorofa nyingi zilizo anguka.”

“Basi muta nikuta hapo. Muonekano wangu ni huu hapa”

Josephine akamkabidhi raisi Mtenzi picha ya jinsi atakavyo kuwa amevalia.

“Haya mavazi ni yako?”

“Ndio ninayo ndani ya begi hapa”

“Ssawa niwatakie kazi nje”

Magreth akaagana na raisi Mtenzi pamoja na Josephine kisha akaondoka eneo hilo, haikumchukau muda mrefu kufika eneo la karibu la majengo hayo yaliyo haribiwa kwa milipuko. Akaificha pikipi yake neo ambalo sio rahisi kwa mtu kuweza kumuona. Akabadilisha nguo zake na kuvaa nguo hiyo ambayo ina uwezo wa kuto kuingiza risasi. Akakoki bastola yake, akahesabu silaha zake zilizo kaa mfumo wa nyota zimapato kumi na mbili kisha akaziweka vizuri. Kisu chake kikali ambacho kime jikunja kidogo mbele na kime unganishwa na mnyororo mrefu, akauzugushia vizuri kionini mwake. Uzuri wa macho yaliyo tengenezwa kwenye nguo yake hiyo yana uwezo wa kuona vizuri kwenye kigi hivyo haikumpa shida kuligagua eneo hilo. Hazikupita dakika ishiri akaanza kusikia ving’ora vya gari za raisi. Magreth akasimama kwenye moja ya gorofa ambayo zipo tano, akashuhudia gari hizi jinsi zinavyo simama eneo la karibu na gorofa hilo. Akashuhudia jinsi walinzi wa raisi wanavyo shuka kwenye gari hiyo huku wakiambatana na Josephine aliye valiashwa jaketi la kuzuia risasi. Wakaanza kutembea kuelekea ndani ya moja ya gorofa kabla hata hawajafika mlipuko mkubwa ukatokea kwenye gorofa hilo na kusababisha walinzi walio kuwa wametangulia mbali kurushwa mbali huku, mzee Mbogo ambaye ana fanania na raisi Mtenzi akimrukia Josephine na kumziba asiweze kuudhurika na vipande hivyo vya mlipuko. Milio ya risasi ikaanza kurindima kuelekea zilipo gar hizo za msafara wa raisi na kumfanya Josephine achanganikiwe na asijue ni wapi aanze kushambulia watu hao ambao wanaonekana wame dhamiria kabisa kumua raisi na kila mmoja aliye fika eneo hilo.

***

Zuma akafika katika mtaa anao ishi Magreth. Akaitazama picha ya nyumba ya Magreth iliyopo kwenye simu yake na akafanikiwa kuiona nyumba hiyo. Akaanza kutembea kuelekea getini huku akiwa amejiandaa vizuri kwa mashambulizi ya aina yote. Akafika getini na kutazama kamera zilizo fungwa eneo hilo. Akaminya kitufe cha kengele huku akisubiria majibu ya kufunguliwa geti hilo. Alipo ona kimya kwa dakika moja, akatoa plasta ngumu na kuibandika kwenye kitufe hicho na kusababisha kengele hiyo kuendelea kujiminya kwa nguvu na kumbuguzi Juma ambaye amekaa sebleni akitazama filamu.

‘Au wame pata matatizo hivyo wana kimbizwa’

Juma alijishauri huku akisimama, akafungua pazi na kuchungulia nje. Akashushusha pumzi taratibu kisha akatoka sebleni hapo.

“Nani”

Juma aliuliza huku akielekea kwenye geti dogo. Zuma akaichomoa bastola yake aliyo kuwa ame funga kiwambo cha kuzuia sauti huku akiamini kwamba huyo anaye uliza ni mlinzi wa nyimba hiyo kwani kwa taarifa alizo nazo ni kwamba nyumba hiyo wana ishi wanawake tu.

“Nani?”

Juma aliuliza kwa msisitizo huku akifungua kitasa cha ndani cha geti hilo. Kitendo cha kufungua geti dogo akakutana uso kwa uso na bomba ya bastola ya Zuma na kumfanya astuke sana na kuanza kurudi nyima huku akitetemeka kwa woga.

“Magreth na Josephine wapo wapi?”

Zuma aliuliza kwa msisitizo huku akimtazama Juma aliye kaa kifua wazi.

“Ha….h….a…ha…wa…po”

Juma alijibu kwa kigugumizi. Zuma hakuwa na huruma yoyote kwa Juma akafyatua risai iliyo mpiga Juma kwenye paji lake la uso na kutokea usogoni na akaanguka mzima mzima na eneo hilo likaanza kutapakaa damu na Zuma akaelekea ndani ya nyumba hiyo kuhakikisha kwamba ana wapata Josephine na Magreth ambao amepewa jukumu la kuwaua na Evans Shika.



Zuma akakagua chumba kimoja baada ya kingine ila hakufanikiwa kumuona mtu yoyote.

“Shitiii”

Zuma alizungumza kwa sauti ya hasira kwa maana alio wafwata hawapo. Akatoa simu yake mfukoni na kumpigia bosi wake.

“Ehee vipi ume fanikiwa?”

Baby Al alizungumza huku akiwa na shahuku ya kuhitaji kufahamu kama ame fanikiwa katika kazi aliyo muagiza.

“Nime mkuta mlinzi tu wahusika hawapo”

“Mmalize huyo mlinzi na uendelee na target namba mbili. Jery na Julieth”

“Sawa mkuu”

Zuma akatoka nje, akautazama mwili wa Juma, akainyanyua miguu yake, akamburuta hadi kwenye bustani ya maua iliopo eneo hilo na kumsukumia hapo kisha akaondoka huku akirudishia geti hilo na sio rahisi kwa mtu kuweza kufahamu kama eneo hilo kuna uvamizi ume tokea.

***

Magreth akatazama watu wanao shambulia msafara huo wa raisi, akachomoa silaha zake zenye muundo wa nyota na kuanza kuzirusha sehemu walipo washambuliaji hao, kila aliyo irusha ilikwenda kwa kasi sana na kila mmoja aliye kutana na silaha hiyo alijikuta akifa ndani ya muda mchache kwa maana silaha hiyo ina sumu kali sana. Magreth akashuka kwenye gorofa hilo kwa kasi sana na kukimbilia eneo ambalo yupo Josephine, mzee Mbogo pamoja na walinzi wengine wanao jaribu kupambana na maadui hao. Magreth akaingia kwenye moja ya gari na kuliendesha kwa kasi hasi mbele ya eneo alipo lala Josephine na mzee Mbogo. Akashuka kwenye gari hilo na kuwafwa sehemu walipo lala.

“Vipi mupo salama”

“Mage”

Josephine alizungumza huku akiwa amejawa na woga mwingi sana.

“Ndio, mupo salama?”

“Ndio”

Mzee Mbogo alijibu

“Ingia naye ndani ya gari na muondoke na walinzi wengine sawa”

“Sawa”

“Magreth na wewe vipi?”

Josephine aliuliza huku akwia na wasiwasi.

“Nina shuhulika nao hawa nyingi nendeni”

“Sawa”

Wakaingia kwenye gari hiyo ambayo haiingizi risasi kiurahisi.

“Lala chini”

Mzee Mbogo alizungumza na Josephine akatii kwa kuinamisha kichwa chini ya gari hilo. Mzee Mbogo akawasha gari hilo na wakaondoka eneo hilo kwa kasi huku walinzi kadhaa wakiungana na mzee Mbogo kuodoka eneo hilo na kurudi ikulu. Wapelelezi wa jeshi la Kimarekani ambao kweli walipanga kumuondoa raisi Mtenzi, wakajikuta wakishangaa kumuona mtu ambaye kila wanavyo jaribu kumshambulia kwa risasi, hafi wala kuanguka chini.

Magreth kama Simba aliye jeruhiwa, hakuogopa kuwafwat wapelelezi hao wa Kimarekani wapatao sita, huku wengine wanne akiwa amesha waua. Magreth akafanikiwa kufika eneo hilo, hakutaka kuuliza alicho anaza kukifanya ni kuanza kupambana kwa kutumia nyororo ambayo mbele ina kisu kikali sana na kimejikunja mithili ya nyengo ya kukatia majani. Endapo ata pitisha kisu hucho mkononi ni lazima aondoke na kipande cha mkono. Wanaume hao walio jazia miili yao kwa misuli na kubarikiwa vimo virefu, wakajitahidi kadri ya uwezo wao kuhakikisha kwamba wana pambana na Magreth ila walijikuta wakishindwa kabisa. Mapamno hayo yaliyo dumu kwa dakika kumi, yalimpa ushindi Magreth huku wapelekezi wanne akiwazimisha huku wawili akiwaua kikatili sana, kwani mmoja ame mkata kichwa chake na mwengine amamkata miguu yote miwli na mikono yote miwili.

“Nime maliza kazi”

Magreth alizungumza kwa kutimia kinasa sauti kilicho sikioni mwake.

“Wanajeshi wana kuja hapo eneo la tukio”

Magreth aliisikia sauti ya raisi Mtenzi.

“Sawa muheshimiwa”

Kikosi maalumu cha jeshi cha special force kikafika eneo hilo. Wakawafunga pingu wapelelezi hao wanne na moja kwa moja wakapelekwa kwenye kambi ya jeshi ya kikso hicho.

“Hongera sana”

Kila mwanajeshi alipo muona Magreth alimpa pongezi japo ame valia mavazi ambayo hajaonyeshi uso wake. Magreth akapanda pikipiki yake na kurudi ikulu, akafika ikulu na moja kwa moja akaelekea ofisini kwa raisi Mtenzi.

“Hongera sana Mage”

Raisi Mtenzi alziungumza kwa furaha huku akimtazama Magreth jinsi alivyo pendeza na nguzo zake hizo.

“Nashukuru muheshimiwa. Ndugu yangu yupo wapi?”

“Yupo chumba cha mapumziko”

“Nina imani wame fika salama”

“Ndio”

“Naweza kwenda kumuona?”

“Ndio”

Magreth akatoka ofisi hapo na akakutana na Jery pamoja na Julieth wakielekea ofisini kwa raisi Mtenzi. Jery na mke wake wakaonekana kumshangaa sana Magreth ila hawakuweza kumjua kwa maana sura yake ime zibwa na nguo hizo.

“Baba huyo tulite kutana naye hapo kwenye kordo amevalia mavazi kama Black Panther ni nani?”

Jery aliuliza mara baada ya kuingia ofisini kwa baba yake.

“Huyo ni Mage”

“Mage gani?”

“Magreth ambaye tulipata naye chakula cha usiku”

Julieth akastuka kidogo.

“Sasa kwa nini ame valia mavazi hayo?”

“Ametoka kufanya kazi ya kijasusi. Huyo binti ni hatari sana”

“Sijakuelewa baba”

Jery aliendelea kuhoji.

“Hizi ni oparesheni za usalama, siwezi kukueleza kila jambo. Ehee niambie ni nini kime waleta huku?”

“Tulifwata na walinzi wako kwa baba mkwe na tume rudishwa ikulu”

“Ndio kwa sasa nchi usalama wake bado haujawa sawa. Sinto hitaji mutoke kuelekea sehemu yoyote kuanzia sasa. Tumeelewana?”

“Ndio baba”

“Ila baba mkwe kesho kutwa tuna wazika kaka yangu. Je siruhusiwi kutoka?”

“Tuta angalia usalama wa hiyo siku”

“Sawa”

“Muna weza kwenda kupumzika. Alafu Julieth ume fikia wapi juu ya ombi niliko kuomba”

“Nipo tayari muheshimiwa”

“Basi kesho asubuhi nita kuomba uweze kujiandaa na uta pewa utaratibu wote”

“Sawa baba”

Jery na mke wake wakatoka ofisini hapo na kuelekea eneo analo ishi raisi. Taratibu Magreth akafungua mlango wa chumba cha kupumzikia, akamkuta Josephine akiwa amejilaza kwenye moja ya sofa.

“Hei”

Magreth aliita kwa sauti ya upole na Josephine kwa haraka akakaa kitako na kumtazama Magreth.

“Ohoo asante Mungu ume rudi salama”

Josephine alizungumza huku akiwa na furaha. Wakakumbatiana kisha wakaka kwenye sofa.

“Mbona ume kuja na nguo hizo?”

“Sikuona haja ya kubadilisha nguo kwa maana eneo lenyewe halikuwa na usalama”

“Ehee ime kuwaje?”

“NIme fanikiwa kuwakamata wanne na wawili wame kufa”

“Ni kina nani?”

“Wale watu wana asili ya Kimarekani ila sifahamu ni kina nani”

“Kwa hiyo hii ishu Wamarekani kumbe wame ifanya kuwa serious sana”

“Ndio hivyo. Vipi tuna lala hapa ikulu au tuna kwenda home?”

“Sijajua, ila tulale hapa ikulu kwa maana masaa yaliyo salia ni machache kufika asubuhi.”

“Sawa, nime choka kwa maana ile mijamaa ina nguvu sana, laiti ninge kuwa sina mbinu za kupambana basi leo hii wange niua”

“Pole rafiki yangu. Alafu nina habari njema”

“Habari gani?”

“Mungu ameamua kutoa swala la sisi kufa ame tupa miaka mingi sana ya kuishi hapa duniani.”

“Wee”

“Haki ya Mungu vile”

Magreth akashusha pumzi huku akiwa amejawa na furaha nyingi sana moyoni mwake.

“Ohoo Mungu ni mwema kwa maana leo nilikuwa nina jua ndio siku yangu ya mwisho kuishi duniani”

“Mungu ana makusudi na sisi”

“Ni kweli. Ule mlango ni wa wapi?”

“Choo na basu”

Magreth akavua nguo hizo na akabakiwa na nguo za ndani tu. Akaingia bafuni hapo na kuanza kuoga taratibu huku akianza kukumbuka matukio ambayo yame toke siku hiyo. Akatoka bafuni hapo kisha akavaa nguo za kawaida alizo ziweka ndani ya begi hilo.

“Hivi ume wasiliana na Juma?”

Magreth alizungumza huku akimtazama Josephine usoni mwake.

“Nilimpigia na kukuta simu yake haipo hewani. Ila nina kumbuka aliiweka chaji chumbani”

“Ahaa sawa, sasa hivi muda umekwenda nina hisi ata kuwa amelala”

“Ni kweli”

Josephine alizungumza kwa amani kabisa pasipo kufahamu kwamba mwanaume anaye mpenda amesha uwawa kikatili.

***

Eneo zima la wanajeshi wa Marekani walio kuja kwa lengo la kutejenga jiji la Dar es Salaama likazungukwa na wanajeshi wa Tanzania kuhakikisha kwamba hakuna anaye toka hadi pale upelelezi wa walio kamatwa kukamilika. Hali ya hatari iliweza kutawala kwa wanajeshi wa pande zote mbili huku kila mmoja wao akiwa tayari kwa mashambulizi yoyote tayakayo tokea kuanzia muda huo. Wapelelezi hao wa kijeshi wa Marekani walio kamatwa, detail zao zote zikafikishwa mezani kwa raisi Mtenzi.

“Kila kitu kupo hapa muheshimiwa”

Mzee Mbogo alizungumza huku akimpa raisi Mtenzi mafaili kumi ya wanajeshi hao ambao ni wapelelezi na walikuwa wame dhamira kabisa kumuu raisi Mtenzi. Raisi Mtenzi akaanza kusoma faili moja baada ya jengine.

“Hawa walio pigiwa tiki ndio wapo hai?”

“Ndio muheshimiwa”

“Mpigieni video call raisi wa Marekani”

“Sawa”

Raisi Mtenzi akakaa mbele ya tv yake na baada ya muda mchache raisi wa Marekani akawa hewani.

“Nina ona ume pitisha masaa ishirini na nne niliyo kupitia na kambi waliyo fikia wanajeshi wangu ime zungukwa na wanajeshi wako, kwa hiyo ume jiandaa kuingia kwenye vita na mimi?”

Raisi wa Marekani alizungumza kwa kujiamini kana kwamba hajui walilo fanya vijana wake.

“Nina imani uta kuwa ume stuka sana kuona nikiwa nipo hai. Hizi ni faili za wanajeshi wao ambao uliwatuma kunishambuli na kuniua. Sasa nina kwenda kufichua siri hii duniani kote ili waijue Marekani ni nchi ya ina gani. Kama mulizoea kupambana na Waarabu na mukawa muna wapiga kijinga basi sasa ume ingia kwenye sehemu ambayo sio ya kinyonge nita rudisha kila shambulizi ambalo utakuwa una lituma kwenye nchi yangu. Umenielwa”

Raisi Mtenzi alizungumza kwa ukali huku akimuonyesha raisi huyo mafaili ya vijana wake ambao aliwapa kazi ya kumua raisi Mtenzi.

“Alafu nikukuumbushe tu, mfumo wangu wa kijeshi huujui na sijawahi kuuweka wazi kama nyinyi munavyo jiweka wazi. Nina weza kutuma watu wakaingia white house yako au wakailipua W.D yako hapo ndipo utakapo elewa ni nguvu gani ambayo Mungu ametupatia sisi Watanzania”

Raisi Mtenzi alizidi kuzungumza kwa kujiamini. Raisi wa Marekani akashusha pumzi huku akimtazama raisi Mtenzi usoni mwake kwa maana endapo ukweli huo utakwenda kufichuliwa baso mataifa ambayo haya Muungu mkono Marekani kama North Korea pamoja na Urusi basi yana weza kuungana na nchi ya Tanzania na wakampatia nguvu ambayo endao wata amua kupambana na Marekani basi ita kuwa ni vita atakayo shindwa kwa asilimia ndogo sana.

“Waachie wanajeshi wangu na warudi nchi na mahusiano ya kimisaada mimi na wewe ita ishia hapo?”

“Mumeua walinzi wangu wanne, nime washililia wapelelezi wako. Wanne na hao ndio wata kuwa ndio ushahidi pekee wa kuwadhihirishia dunia kwamba nyinyi bado muna taka kuendelea ukoloni wa kuzitesa nchi nyonge, japo zina uongozi wao ila nyinyi muna hitaji kwa juu ya nchi hizo ila kwa Tanzania hilo jambo lita kuwa ni ndoto”

Raisi Mtenzi mara baada ya kuzungumza maneno hayo akakta mazungumzo hayo kwa kuzima tv. Akachukua simu yake ya mezani na kumpigia mkuu wa majeshi.

“Ndio muheshimiwa”

“Hakikisheni hatokki mwananjeshi hata mmoja wa Kimarekani na endapo wata dhubutu kutoka waueni wote”

“Sawa muheshimiwa”

Raisi Mtenzi akakata simu na kumtazama mzee Mbogo pamoja na mr the Brain ambao wame muunga mkono raisi kwa maamuzi hayo ya kijasiri.

“Muheshimiwa nina wazo”

Mzee Mbogo alizungumza kwa sauti ya upole.

“Niambie”

“Una onaje huyu binti Magreth tuka mpatia nafasi kwenye kitengo cha usalama wa nchi kwa maana yupo vizuri muheshimiwa. Kuwahimili wapelelezi kumi, huku wawili akiwaua na wanne kuwakamata sio jambo la kawaida.”

“Ni kweli ana kitu cha kipekee ambacho laiti kama tunge kijua hapo awali basi tusinge kuwa tuna pata shida kwenye mambo madogo madogo”

“Ni kweli, muheshimiwa”

“Hivi hao wapelelezi wengine wanne waliuwawa na walinzi wangu?”

“Ndio muheshimiwa”

“Basi hakikisheni kwamba mipaka yetu yote ya nchi ulinzi una imarishwa. Baharini pia ulinzi una imarishwa vizuri na anga, Endapo ita pita ndege isiyo na maelezo kwenye anga la Tanzania ishushwe tume elewana”

“Ndio muheshimiwa raisi”

“Kazi nzuri muna weza kwenda kupumzika sasa”

Mzee Mbogo na mr the Brain wakatoka ofisi hapo. Raisi Mtenzi akafunga mafaili muhimu kisha akatoka ofisini hapa kwa maana muda ume kwenda sana. Kalba hajaelekea nyumban kwake akapitia katika chumba walipo Josephine na Magreth. Akakaribishwa na Josephine, raisi Mtenzi akaingia ndani huku akiwa amejawa na tabasamu pana.

“Nime wasumbua?”

“Hapana muheshimiwa”

“Kusema kweli nina washukuru sana kwa kila mulilo lufanya kwa ajili ya nchi hii. Muna weza kuhisi na mambo madogo sana ila ukweli ni kwamba mume nipatia nguvu ya kuweza kusimama na kuwaeleza ukweli watu wa dunia hii ni kitu gani kunacho endelea kati yetu na Marekani. Asanteni sana”

“Nasi tuna shukuru muheshimiwa kwa nasafi hii ambayo ume tupatia”

Josephine alijibu huku akiwa na furaha sana.

“Mage nina ombi kwako”

“Ombi gani muhshimiwa”

“Nina kuomba uweze kuingia kwenye kitengo cha usalama wa taifa”

Magreth akamtazama Josephine aliye mkonyoza akishiria kwmaba akubali nafasi hiyo adimu aliyo pewa.

“Mmm naomba nafasi ya kufikiria muheshimiwa”

“Basi fikiria alafu unipatie jibu”

“Sawa mkuu”

“Niwatakie usiku mwema na Josephine kesho una kumbuka kwamba una anza kazi?”

“Ndio mueshimiwa”

“Haya”

Raisi Jery akatoka ndani hapo na kuwaacha Josephine wakiwa na furaha.

“Mage kubali kuwa mwana usalama”

“Mmmm acha nijifikirie kwanza kwa maana mimi nime zoea kujituma na kufanya biashara zangu mimi mwenyenye sasa linapo kuja swala la kuajiriwa tena kwenye mambo kama hayo ya usalama huwa nina ogopa sana”

Magreth alizungumza huku akitoa simu yake kwenye begi. Magreth akastuka kidogo mara baada ya kuona notification kwenye simu yake ikimuashiria kwamba geti la nyumbani kwake lipo open.

‘Ina maana Juma hajafunga geti?’

Magreth alijiuliza kimoyo moyo huku akiingia upande wa video zilizo rekodiwa. Akaanza kutazama video ya kuanzia muda geti lilipo achwa wazi. Magreth akastuka sana mara baada ya kumuona mwanaume mmoja aliye valia kofia, akiminya kitufe cha geti lake, kisha akakifunga kitufe cha kengele hiyo wa plasta. Kitendo hicho kikamuashiria kabisa Magreth kwamba mtu huyo sio salama. Mapigo ya moyo yakazidi kumuenda kasi mara baada ya kumuona Juma akifungua geti hilo, hakuweza kusikia walicho kuwa wana kizungumza ila akahisi moyo ukimlipuka mara baada ya kushuhudia Juma akipigwa risasi ya kichwa jambo lililo mfanya mwili mzima kumuisha nguvu. Akamtazama Josephine aliye lalala kwenye sofa jengine huku akiwa amevalia headphone masikoni mwake, akamuonea huruma sana kwa maana hajui ata jisikiaje pale atakapo pata habari kwamba mwanaume anaye mpenda amefariki duniani.



Josephine kwa haraka akakurupuka kwenye sofa alilo lala, akakaa kitako na kuvua headphone zake.

“Mage”

“Mmmmm”

Magreth aliitikia huku akijaribu kuficha majonzi yake.

“Hivi Juma una hisi ni mwanaume sahihi wa kunia?”

Swali la Joseohine likamfanya Magreth kubaki na mshangao huku akikosa cha kuzungumza.

“Aha….kwa….kwa nini una uliza?”

“Kwa sababu wewe una mfahamu na kumjua vizuri”

Magreth akazima kabisa simu yake na kuirudisha ndani ya begi lake.

“Mage upo sawa?”

“Yaa nipo sawa”

Magreth alizungumza huku akijilaza kiunyonge kwenye sofa hilo.

“Hapana Mage nina kufahamu haupo sawa”

Josephine alizungumza huku akimfwata Magret sehemu alipo lala, akamshika eneo la shingoni mwake na kukutaa akiwa na joto kali sana.

“Mungu wangu. Mage una umwa wewe”

“Nipo sawa Jose”

“Hapana una umwa, hii homa uliyo kuwa nayo ni kali sana ngoja nikakutafutie dawa, huwezi kulala hivyo”

Josephine akatoka ndani hapo na kumfanya Magreth kuanza kulia kwa uchungu sana.

“No siwezi kukaa hapa”

Magreth alizungumza akisimamam, akavaa mgongoni begi lake hilo, akavaa na kiatu vyake na kuelekea mlangoni, kitendo cha kushika kitasa mlango ukafunguliwa na Josephine akaingia huku akiwa ameongozana na daktari wa ikuku.

“Mage una kwenda wapi?”

“Jose nakuomba nika shuhulikie jambo moja muhimu sana”

“Hapana bwana, hembu acha kwanza daktari akutazame, dokta hembu muangalie rafiki yangu ana onekana ana umwa kabisa huyu”

Josephine alizungumza huku akimshika mkono Magreth na akamlazimisha kurudi ndani hapo.

“Mage natambua kwamba matukio uliyo yafanya leo kidogo yana kuweka katika wakati mgumu. Hembu tulia kwanza dokta akuhudumie ili afya yako iwe sawa”

“Nina hitaji kuonana na raisi sasa hivi”

“Mage sasa hivi ni usiku nina hisi kwamba raisi ata kuwa ame lala”

“Jose wewe si una kwenda kuwa chief staff. Nisaidie nimuone raisi sasa hivi, la sivyo sinto kubali kuhudumiwa”

Dokta akastuka mara baada ya kusikIa kwamba binti huyo ana kuwa chief staff.

“Sawa nina kwenda kumuia raisi, ia dokta muhudumie”

“Sawa muheshimiwa”

Dokta alizungumza kwa heshima, kisha Josephine akatoka ndani hapo. Dokta akaanza kumpima Magreth joto lake.

“Una homa kali, nita kupa vidonge tu vya kushusha joto kama hadi asubuhi hali ita kuwa sio nzuri basi tuta fanya vipimo vingine zaidi”

“Sawa, nipatie tu hiyo dawa”

“Ipo kule kwenye hospitali ya ikulu, kama huto jali tuna weza kuongozana na kwenda kuichukua.”

“No kaniletee”

Dokta akamtazama Magreth jinsi anavyo zungumza kwa msisiztizo kisha akatoka ndani hapo. Raisi Mtenzi na Josephine wakaingia ofisini hapo huku raisi akionekana kuwa na wasiwasi.

“Vipi hali yako, dokta amekupatia matibabu?”

Raisi Mtenzi alihoji huku akiwa amejawa na wasiwasi mwingi sana.

“Dokta ame kwenda kunichukulia dawa, ni homa ya kawaida tu”

“Ohoo asante Mungu”

“Muheshimiwa nina hitaji tuzungumze mimi na wewe”

“Hapa”

“Hapana ofisini kwako”

“Basi twende”

Magreth akafungua begi lake na kutoa simu yake.

“Jose dokta akija muambie anifwate ofisini kwa raisi”

“Sawa ila kuwa makini”

“Pao”

Wakatoka ndani hapo kwa bahati nzuri wakakutana na daktari kwenye kordo. Dokta akampatia Magreth dawa hizo pamoja na chupa ya maji ya kunywa.

“Meza vidonge viwili kutwa mara mbili”

“Sawa”

Raisi Mtenzi na Magreth wakaingia kwenye ofisi, Magreth akameza vidonge hivyo kisha akawasha simu yake.

“Kuna nini Mage nime stuka snaa kusikia kwamba una umwa”

“Siumwi kama Josephine anavyo fikiria, nina imani kwamba endapo Josephine ataipata habari hii ana weza kuuwa zaidi ya jinsi ninavyo umwa kichwa”

“Habari! Habari gani?”

Magreth akaiweka video hiyo ya mauaji ya Juma kisha akamkabidhi raisi Mtenzi simu yake. Raisi Mtenzi akaanza

kutazama video hiyo na kumfanya astuke kidogo kwa maana kijana huyo ana mtambua.

“Mungu wangu!! Huyu si yule kijana wako?”

“Ndio ni yeye na hiyo video ni ya usiku huu na imerekodiwa majira ya saa sita usiku na cctv kamera za pale nyumbani kwangu. Mbaya ni kwamba huyu ni mwanaume ambaye ame uteka sana moyo wa Josephine na endapo ata tambua kwamba ame kufa, hata hiyo nafasi yako ambayo una taka kumpatia hapo kesho hato kubaliana nayo”

Raisi Mtenzi akashusha pumzi huku akikaa kwenye kiti chake.

“Sasa ime kuwaje ame uwawa, tatizo ni nini?”

“Huyu mtu anavyo onekana hakuja hapo kwa ajili ya Juma. Alikuja nyumbani hapo kwa ajili yangu na Josephine”

“Masikini wa watu, kijana wa watu ame fariki akiwa bado mdogo sana”

“Ndio hivyo muheshimiwa ninacho kihitaji mimi ni kuanza kudili na hawa watu”

“Una wafahamu?”

“Siwafahamu, ila nina kuomba unipe msaada wa vijana wako wa mambo ya mtandao wahakikishe kwamba wana nitafutia details za huyu mtu usiku huu huu”

Magreth alizungumza kwa msisitizo huku akimtazama raisi Mtenzi usoni mwake.

“Sawa nita fanya hivyo. Acha niwasiliane na askari waweze kufika eneo la tukio”

“Sawa”

Raisi Mtenzi akampigia simu RPC Karata na kumuagiza aweze kwenda kwenye nyumbani kwa Magreth.

“Twende kwenye chumba cha mawasiliano”

Raisi Mtenzi na Magreth wakatoka ndani hapo, Wakaingia kwenye chumba hicho chenye wafanyakazi zaidi ya hamsini ambao wana fanya kazi usiku na mchana.

“Hii ni eneo ambalo oparesheni zote za kiusalama zina endeshewa hapa”

Raisi Mtenzi alizungumza huku akimtazam Magreth usoni mwake.

“Sawa sawa muheshimiwa”

Raisi Mtenzi akamkabidhi kijana mmoja simu ya Magreth na akaihamisha video hiyo.

“Si muna weza kuzipata detail zake?”

“Ndio muheshimiwa dakika moja”

Kijana huyo akaanza kuminya minya keybord ya computer kwa kasi, ndani ya sekunde kadhaa akapata taarifa za mtu huyo.

“Ana itwa Zuma Zuma. Ni mlinzi wa karibu wa binti huyu anaitwa Baby Al”

Kijana huyo alizungumza huku akimtazama raisi Mtenzi pamoja na Magreth usoni mwake.

“Mwaka 2003 hadi 2009 alikuwa ni komandoo wa nchi ya Ufaransa, baada ya kuacha kazi detail zake hakuanzia hapo zinaonyesha ni kwamba alisha fanya kazi katika kitengo cha Interpol kwa miaka miaka miwili na baada ya hapo akaanza kumlinda huyo binti anaye itwa Baby Al.

“Huyo Baby Al ni nani?”

Magreth aliuliza.

“Ngoja kwanza”

Kijana huyo akatafuta taarifa za Baby Al na akafanikiwa kuzipata.

“Baby Al, jina lake halisi ana itwa Chariry Griziman ni raia wa Ufaransa. Pia ni mfanya biashara wa mafuta na baba yake ni mmoja wa matajiri wakubwa na waziri mkuu wa Ufaransa bwana Griziman Laurance.”

“Sasa ni kwa nini mlinzi wake ana tuwinda sisi?”

Magreth aliuliza huku akiwa amejawa na mshangao mkubwa sana usoni mwake.

“Ngoja kwanza”

Kijana huyo alizungumza na kuendelea kutafuta sana. Akapata picha moja ya siri ya Baby Al akiwa amepiga na kiongozi wa kundi la Al-Shabab.

“Mkuu huyu binti kwa namna moja ama nyingine anafanya kazi na kundi hilo la Al-Shabab.”

Kijana huyo alizungumza huku akiikuza picha hiyo kwenye computer yake yeye kioo kikubwa cha inch 32.

“Shiti ina bidi tudili na huyo mwanamke”

Raisi Mtenzi alizungumza kwa msisitizo.

“Masaa arobaini na nane yaliyo pita alikuwa Zanzibar na meli yake ya mizigo na amekaa nchini Tanzania kwa miezi miwili”

“Mungu wangu uta kuta ame weza kuendesha zoezi zima la milipuko ya jiji la Dar es Salaam?”

Raisi Mtenzi alizungumza huku akiwa akiitazama video hiyo.

“Nina hisi hivyo muheshimiwa. Ngoja kwanza mkuu”

Kijana huyo alizungumza huku akiendelea kufukunua taarifa za siri za Baby Al. Kijana huyo akaonyesha picha za cctv kamera zilizopo katika eneo la maegesho ya magari ya bandari ya Zanzibar.

“Huyu mpumbavu ndio muhisika”

Magreth alizungumza kwa hasira mara baada ya kumuona Baby Al akiwa ameshikama mkono na Evans.

“Una maanga gani kwamba huyu ni muhisika?”

Raisi Mtenzi auliuliza huku akimtazama Magreth usoni mwake.

“Josephine aliweza kutabiri juu ya vifo vyetu mimi na yeye. Akasema kwamba Evans ameweza kuwalipa wata pesa kwa ajili ya kutuua. Sasa nina imani kwamba huyo ndio aliye pewa jukumu la kuwaua na Evans ndio aliye toa agizo hilo”

“Huyo Evans ndio nani?”

“Alikuwa X boy friend wangu”

“Sasa kwa nini ana taka kuwaua wewe na Josephine?”

“Sija fahamu”

“Ina bidi akamatwe mara moja huyo kijana ni mshenzi sana”

Raisi Mtenzi alizungumza kwa msisitizo.

“Fredy si bado wapo Zanzibar?”

“Hapana hiyo meli ilisha ondoka masaa zaidi stini sasa”

“Nina imani bado ita kuwa kwenye ukanda wa Tanzania?”

“Sina uhakika muheshimiwa”

“Hembu jaribu kuitafuta kwa kutumia satelaite”

“Sawa muheshimiwa”

Fredy akaendelea kuitafuta meli ihyo ili kuhakikisha kwamba kama bado ipo kwenye ukanda wa nchi Tanzania basi waweze kuizuia na kuhakikisha kwamba wana wakamata waalifu wote.

***

“Kazi yako ina kwenda kukamilika hivi karibuni”

Baby Al alizungumza huku akimtazama Evans aliye kaa kwenye moya kiti huku mikono na miguu yake ikiwa ime fungwa pingu pamoja na minyororo.

“Sawa, ila samahani Baby Al, mimi sio mfungwa na wala sio mtu mbaya kwako sasa kwa nini una nichukulia kama muhalifu”

Baby Al akatabasamu kisha taratibu akanyanyuka huku akivuta sigarate yake. Akamsogelea Evans sehemu alipo kaa na kumtazama kwa macho ya kumchunguza. Akavuta fumba kubwa la moshi kisha taratihbu akampulizia Evans usoni mwake na kumfanya aanze kukohoa.

“Hahaaa hukuwahi kuvuta kiti kama hichi”

“Ha…aha…hapana”

Baby Al akavuta tena moshi mkubwa kisha akamzisogelea lipsi za Evans na kuzikutanisha na lipsi zake, taratibu akaanza kuusukumizia moshi huyo wa sigara mdomoni mwa Evans na kumfanya azidi kuchachawa kwa maana toka kuzaliwa kwake hakuwahi kuvuta sigara.

“Uta niua”

Evans alizungumza kwa shida huku macho yake yakizidi kuwa mekundu. Baby Al akaushusha mkono wake wa kulia kwenye pamaja ya Evans na taratibu akausogeza hadi kwenye jogoo wake. Akaanza kuupapasa taratibu na kumfanya Evansa aanze kujawa na hisia kali za mapenzi. Mtomaso huyo wa Baby Al, ukamfanya Jogoo wa Evans kusimama kama msubari. Baby Al, akafungua zipi ya suruali hiyo ya Evans na kumtoa jogoo huyo.

“Woooo Watanzania mume barikiwa mashine”

Evans akakosa cha kuzungumza zaidi ya kukaa kimya. Baby Al akaanza kumchua taratibu jogoo huyo na kumfanya Evans kuhisi raha sana, kiasi cha kumfanya afumbe macho yake. Taratibu Baby Al, akaizima sigarate yake na kuanza kumuingiza mdomoni jogoo wa Evans.

“Ohoo…aiiisiiia….iii…oooa”

Evans alilalama huku akianza kusahau shida na mateso aliyo patiwa na msichana huyo. Baby Al naye hisia za kimapenzi zikamchukua na kujikuta akisahau majukumu yake. Akavua suruali yake, kwa haraka akajipaka mate kwenye kitubua chake kisha taratibu akamkalia Evans pamajani mwake huku akisikilizia jinsi jogoo huyo aliye shiba kisawa sawa anavyo chanja mbuga ndani ya kitumbua chake. Baby Al akaaza kujihudumia huku akihakikisha kwamba ana ikata kiu yake ya kipindi kirefu kwani katika maisha yake amekuwa ni mtu wa kuto wapenda wanaume kabisa.

“Ohoo ohooaiiissiii….aiia….”

Baby Al aliendelea kujipa raha ambazo hata Evans kwa upande wake aliendelea kutoa migoni kwani mwana dada huyo japo ana asili ya kizungu ila michezo ya kukata mauno ana iweza kama Mzaramo tena wa uswahilini.

“Nifungue nikufurahishe”

Evans alizungumza na Baby Al kwa haraka akachukua funguo ya pingu na mnyororo huo na akamfungua Evans. Evans kwa haraka akambabe Baby Al na kumlaza mezani na kuendelea kumpa kichapo mithili ya mbwa dume mwenye ukame. Baby Al alizidi kuchanganyikiwa kwa maana hakuwahi kukutana na mwanaume wa shoka kama Evans, kila aina ya mapigo ya kuhakikisha ana ikuna G spot yake Evans alifanya. Kwa mara nne mfululizo Baby Al alijikute akifika kileleni pasipo hata Evans kufika.

“Ni mkao gani nikae ukojoe?”

Baby Al uzalendo ulimshinda na kujikuta akiuliza swali kwa maana kitumbua chake kina waka moto kwani si kwa mkong’oto huo anao pewa.

“Bana miguu kwa upande?

Evans alizungumza na Baby Al akatii, akaibana miguu yake na kujikunja mithili ya samaniki anaye kunjwa. Evans akaendelea kupelekea moto ulio mfanya kuhisi raha ya ajabu ambayo ndani ya muda mchache akajikuta akiwafyatua waarabu weupe ambao wote wakazama katuka kitumbua cha Baby Al.

“Haki ya Mungu sijawahi kufanywa kama hivi toka nijue mbo** ya mwanaume”

“Kweli?”

“Ndio, ume nipa kitu ambacho nilikikosa kwa wanaume nilio tembea nao.”

Baby Al alizungumza huku wote wakimwagikwa na jasho jingi.

“Usijali uta kuwa una pata haya mambo kila siku”

“Kweli?”

“Ndio”

“Hujaja kunipeleleza wewe?”

“Kwa nini nikupeleleze ikiwa nime kulipa pesa kwa ajili ya kunisaidia kuwaua watu nilio agiza wafe”

Kwa kauli hiyo ya Evans Baby Al akanza kumuamini Evans kwa maana kama engekuwa ni mpelelezi asinge lipa kiasi hicho cha pesa kwa ajili ya mtoto wa raisi kuuwawa.

“Nakupa nafasi kwenye maisha yangu. Ila endapo uta niletea upumbavu nita kuua kwa kukukata huo ubo** wako. Tume elewana Evans”

“Usijali haiwezi kutokea”

“Wewe sema kwamba haiwezi kutokea ila ikitokea nina kuhakikishia kwamba uta jutia ni kwa nini ume nifahamu”

Mlango wa chumba hicho ukagongwa na kuwafanya Evans na Baby Al kuanza kuvaa kwa haraka nguo zao kisha Baby Al akausogela mlango huo kwa ajili ya kumsikiliza huyo anaye gonga mlango.

“Mkuu samahani kuna tatizo kubwa sana una hitajika sasa hivi”

Kijana huyo aliye valia mavazi meusi huku mkononi mwake akiwa ameshika bunduki alizungumza kwa uharaka huku akionekana akiwa na wasiwasi mkubwa sana jambo lililo mfanya Baby Al na Evans anaye sikia mazungumzo hayo kustuka sana.



“Nina kuja”

Baby Al akafunga mlango huo na kumgeukia Evans.

“Usitoke humu ndani, ume nielewa?”

“Ndio”

Baby Al akafungua mlango na wakaongozana na kijana wake huyo hadi kwenye chumba cha nahodha.

“Muheshimiwa data zetu zime weza kudukuliwa”

Kijana anaye shuhulika na maswala ya mawasiliano na tecnolojia alizungumza huku akimtazama Baby Al usoni mwake.

“Na nani ambaye eme hack?”

“Yame dukuliwa na ikulu ya nchi ya Tanzania na hivi sasa wana jaribu kutafuta location yetu ilipo ila tume weza kufunga kila kitu na hawato weza kutuona.

“Ime kuwaje hadi wa hack system yetu”

“Nime weza kupata moja ya data kwa mtu anaye hack ni hii video”

Kijana huyo mwenye uwezo mkubwa sana kwenye mambo ya tecnolojia alizungumza huku akiweka video iliyo rekodiwa nyumbani kwa Magreth ikumuonyesha Zuma jinsi alivyo kuwa akimuua Juma.

“Shiti”

Baby Al alizungumza huku akiwa na hasir.

“Zuma ndio amesababisha tuweze kuwa target na serikali ya Tanzania”

“Nini walicho weza kukijua kwangu”

Kijana huyo akaminya moja ya faili na kuonyesha kila kitu kilicho somwa kuhusiana na Baby Al na pia akamuonyesha baadhi ya picha zake akiwa na Evans eneo la mapokezi katika bandari ya Zanzibari.

“Mkuu kwani Zuma ame kwenda kufanya kazi gani Tanzania ikiwa tulikuwa naye ndani ya meli”

Baby Al akashindwa kulijibu swali hilo kwa maana kazi aliyo mtuma Zuma kwenda kuifanya ni wao wenyewe ndio walio ipanga.

“Hakikisha una nifahamisha kila kitu kinacho endelea ume nielewa”

“Sawa mkuu”

“Huyo kijana naye taarifa zake ni zipi?”

“Naye ana tafutwa na serikali ya Tanzania”

“Okay”

Baby Al akatoka ndani hapo pasipo kutoa maamuzi yoyote. Akaingia kwenye chumba alicho muacha Evans.

“Serikali ya Tanzania ina kutafuta”

“Kivipi?”

“Ina kutafuta kama mtuhimiwa. Wame fahamu kila kitu kuhusiana na sisi pamoja na kuhusiana na wewe”

“Wamejuaje ikiwa hakuna mtu aliye waambia?”

“Wame weza kudaka video ya Zuma akiwa ana muua mmoja wa kijana aliye kutwa nyumbani kwa Magreth nahisi ata kuwa ni mlinzi”

“Sasa wakimkamata Zuma ita kuwaje?”

“Haito kuwa ni jambo rahisi kumkamata. Zuma ni kombandoo na ana uwezo wa kujilinda yeye mwenyewe na hato weza kurudi hadi ahakikishe kwamba kazi ina kwisha”

“Sawa”

Evans aliitikia kwa sauti ya upole kwa maana hana kauli yoyote ya maamuzi mbele ya Baby Al.

***

“Mwili wa Juma una pelekwa Muhimbili sasa hivi”

Raisi Mtenzi alimuambia Magreth mara baada ya kumaliza kuzungumza na simu.

“Nina weza kwenda kuuona”

“Ndio ila ina bidi kumueleza ukweli Josephine, kwa maana tukishindwa kumuambia ukweli na akaonyeshwa na Mungu lazima ata jisikia vibaya”

Ushauri wa raisi Mtenzi ukamfanya Magreth kukaa kimya kwa sekunde kadha ahuku akiwaza ni namna gani ambavyo ana weza kuzungumza na rafiki yake huyo.

“Huo ni mtihani muheshimiwa, mimi nita shindwa”

“Mimi nita ongea naye. Nipe simu yake na baki hapa”

“Sawa”

Raisi Mtenzi akatoka katika chumba hicho cha mawasiliano na kuelekea katika chumba ambacho Josephine eme pumzika. Akagonga mlango na haikupita hata dakika moja mlango ukafunguliwa.

“Muheshimiwa”

Josephine alizungumza huku akiwa ametawaliwa na tabasamu pana usoni mwake.

“Nime kusumbua?”

“Hapana muheshimiwa vipi Mage yupo wapi?”

“Yupo ofisini kwangu. Tuna weza kuzungumza?”

“Ndio tuna weza kuzungumza”

Raisi Mtenzi akaingia ndani hapo na kukaa kwenye moja ya sofa.

“Ahaa Josephine”

“Ndio muheshimiwa”

“Kuna taarifa hapa nina kuomba uweze kuipokea kwa maana ni tukio lililo tokea usiku wa leo”

“Taarifa gani hiyo muheshimiwa, je ni taarifa mbaya?”

“Yaa ni taarifa mbaya kidogo”

“Mmmm kama ni mbaya acha kwanza kunipatia usiku huu. Ila vipi Magreth yupo salama”

“Ndio yupo salama kabisa”

Josephine akashusha pumzi kidogo kisha akamtazama raisi Mtenzi usoni mwake.

“Ehee niambie hiyo taarifa?”

“Kuna msiba”

“Msiba wa nani tena!!?”

Josephine alizungumza huku akiwa amejawa na mstuko mkubwa sana.

“Juma ame fariki”

“Juma gani?”

Josephine aliuliza huku akiwa hajastuka kabisa kwa maana ana amini kama ni Juma wake yupo nyumbani ame lala muda.

“Jume mpenzi wako”

“Hahahaaa muheshimiwa acha kunitania bwana”

Josephine alijikuta akicheka huku akimtazama raisi. Taratibu raisi Mtenzi akamkabidhi Josephine simu ya Magreth. Josephine akaanza kuitazama video hiyo, akairudia rudia zaidi ya mara kumi kisha akamkabidhi raisi Mtenzi simu hiyo.

“Samahani muheshimiwa nina kuomba unipishe”

Josephine alizungumza kwa sauti ya upole na raisi Mtenzi hakuleta ubishi wowote. Akanyanyuka na kutoka ndani hapo. Josephine akapiga magoti chini na kuanza kusali huku akilia kwa uchungu sana. Mwanaume ambaye aliweka tumaini kwamba ata kuwa ndio mume wake wa maisha yote hadi kifo, leo hii emekufa kwa kuuwawa pasipo sababu yoyote. Josephine akendelea kuomba na kumlilia Mungu hadi ina timia saa kumi na mbili na nusu asubihi, akafumbua macho yake na kunyanyuka huku moyoni mwake akiwa na amani na furata. Uchungu na maumivu yote aliyo kuwa nayo yame ondoka kabisa.

‘Asante Mungu’

Josephine alizungumza huku akijinyoosha viongo vyake ya mwili. Akatoka ndani hapo na kuelekea katika ofisi ya raisi Mtenzi kwa bahati nzuri akamkuta Magreth akiwa amejilaza kwenye sofa la humo ndani.

“Jose”

“Mmmm”

“Amka”

Josephine alizungumza huku akiwa kawaida sana hadi Magreth akashangaa kidogo.

“Saa ngapi sasa hivi?”

“Mmm saa kumi na mbili na dakik arobaini na mbili”

“Aha anime chelewa”

“Kwenda wapi?”

Swali la Josephine kidogo likamuweka njia panda Magreth na kujikuta akikakaa kimya huku akimtazama Josephine usoni mwake.

“Usijali Mage natambua kwamba Juma ame kufa, ila ni kwa makusudi ya Mungu na baada ya kulifahamu hilo nime pata amani moyoni mwangu na furaha yangu ime rejea kama kawaida”

“Sija kuelewa?”

“Juma amekufa kwa ajili yetu. Vifo ambavyo vilikuwa ni kwa ajili yetu Juma ame vibeba yeye hivyo kuwa na amani. Tuandae tararibu za mazishi na tumpeleke nyumbani kwao Tanga”

Zungmza ya kawaida ya Josephine kidogo ikampa matumaini Magreth, japo ni msimba mkubwa sana kwenye maisha yake, ila hakuwa na jinsi zaidi ya kukubaliana na hali halisi kwa maana hawezi kurudisha masaa nyuma na kuyaokoa maisha ya Juma.

***

Hadi kuna pambazuka, Julieth hakupata usingizi kabisa. Muda wake mwingi ana mfikiria Magreth ambaye alipishana naye akiwa amevalia mavazi ya ajabu.

“Baby”

Julieth alimuita Jery ambaye bado yupo usingizini.

“Mmmm”

“Make mume wangu, kume pambazuka”

“Saa ngapi sasa hivi?”

“Saa moja kasoro asubuhi”

“Duuu”

Taratibu Julieth akambusu Jery mdomoni mwake kisha akaka kitandani huku akipiga miyayo ya usingizi.

“Mume wangu una weza kunitafutia picha ya Magreth akiwa akiwa amevalia yale mavazi yake”

“Mmmm!! Lakini jana si uliweza kumuona kwa macho picha ya nini sasa?”

“Nahitaji tu kumuona”

“Ahaa achana naye bwana. Kwanza si una kumbuka kwamba leo ni siku yako ya kuanza kazi”

“Ni kweli ngoja nijiandae kisha niandae kifungua kinywa”

“Sawa mke wangu, acha nilale kidogo kisha uta niamsha. Sawa”

“Mmmmm amka bwana ufanya mazoezi acha uvivu”

“Nina lala kidogo tu bwana”

Jery akavuta shuka hilo na kujifunika gubigubi. Julieth akamtazama kwa sekunde kadha akatabasamu kisha akashuka kitandani hapo. Akaandaa kifungua kinywa haraka haraka, kisha akakindaa mezani, akajianda kwa kuvalia suti nzuri ambayo ime mkaa vizuri mwili mwake. Akamkaribisha baba mkwe wake ambaye naye kwa siku hiyo alichelewa kuamka kutokana na uchovu wa kazi za usiku.

“Baba mbona una onekana kujawa na mawazo”

Jery alimuuliza baba yake huku akiendelea kushindilia mikate iliyo andaliwa vizuri na Julieth.

“Nipo kwenye kipindi kigumu sana katuka uongozi wangu. Nchi ina nihitaji na huku nina tamani kupumzika kwa ajili ya kumzika mke wangu. Hivyo nina jikuta nikiwa katika wakati mgumu sana”

“Pole sana baba ya kwisha”

Julieth naye alizungumza.

“Usijali mwanangu. Mungu ni mwema, pia nina imani muta shirikiana sana katika kuhakikisha muna nishauri mambo mazuri ili nchi isiweze kupitia kipindi kingine kigumu kama hichi tulicho kuwa nacho sasa hivi”

“Amen”

Julieth na raisi Mtenzi wakamaliza kupata kifungua kinywa na kuelekea ofisini kwake. Akamkuta Josephine na Magreth wakimsubiria.

“Kumbe mupo?”

“Ndio muheshimiwa, tulikuwa tuna kusubiria”

Josephine alijibu huku akiwa na furaha kubwa sana hadi raisi Mtenzi akashangaa kidogo. Akamtazama Magreth ambaye naye aliweza kuutambua mshangao huo wa raisi Mtenzi.

“Ahaa poleni kwa kunisubiria. Ila Josephine kabla hatujaanza siki ina bidi niweze kuwatangazia wafanyakazi wote wa ikulu juu ya uwepo wako, sambaba na mkwe wangu hapa Julieth Sanga”

“Sawa muheshimiwa”

“Julieth huyo Josephine nime mtea kuwa ni mtendaji mkuu wa Ikulu na ofisi yangu, yaani Chieff Staff. Pia uta kuwa chini yake”

Julieth akastuka sana moyoni mwake ila hakuhitaji kuonyesha mstuko huo usoni mwake ila kwa namna moja ama nyingine hajapenda kufanya kazi kabisa na Josephine katika ofisi hiyo tena akiwa ndio mkuu wake wa kazi.

“Josephine, Julieth na wale wazee wawili wa jana watakua chini yako na nyote muta kuwa munashirikiana katika kunishauri”

“Sawa muheshimiwa”

Julieth lizungumza huku akiwa na tabasamu feki.

“Basi sawa twendeni nikawatambulishe kwa wafanyakazi wengine”

Raisi Mtenzi akawasiliana na sekretari wake na kumpa jukumu la kuwataarifa wafanyakazi wote kukutana katika ukumbi wa mikutano. Baada ya dakika kumi raisi Mtenzi akaingia katika ukumbi huo huku akiwa ameongozanana Josephine pamoja na Julieth. Akawatambulisha mbele ya wafanyakazi wote na kila mfanyakazi alikubaliana na uteuzi huo kisha kila mfanyakazi akaendelea na majukumu yake. Raisi Mtenzi akawatambeza Julieth katika ofisi zao pamoja na sehemu muhimu za hapo ikulu na kila mmoja akamkabidhi ofisi yake. Julieth hakuwa na amani kabisa kwani moyoni mwake ukiachilia mbali kuchukizwa na kufanya kazi na Josephine ila ana mfikiria Magreth ambaye ni adui yake. Josephine akamuita sekretari wake na kumuomba aweze kumtafutia kijana wa mawasiliano hapo Ikulu. Sekretari akarudi ofisini hapo akiwa ameongozana na kijana wa mawasiliano. Akamuomba aweze kueletewa video ya Magreth jinsi alivyo kuwa amevaa mavazi yake. Kijana huyo hakuwa na pingamizi lolote, ndani ya dakika tano akamtumia Julieth video ya Magreth iliyo rekodiwa na CCTV Kamera akiwa ana tembea kwenye kordo ya hapo ikulu. Josephine kwa haraka akamtumia video hiyo baba yake kwa maana ana kumbuka usiku wa kuamkia harusi yake, baba yake na mama yake waliweza kutapeliwa kiasi kikubwa sana cha pesa.

Nabii Sanga akastuka snaa mara baada ya kuona video hiyo iliyo toka kwa mwanaye Julieth.

‘Baba una mfahamu huyo’

Nabii Sanga liisoma meseji hiyo kisha akaijibu.

‘Huyu ndio yule alitye tuteka na kuchukua pesa zetu’

‘Una jua ni nani?’

‘Hapana ni nani?’

‘Ni Magreth’

Nabii Sanga macho yakamtoka sana huku hasira ya kuzifikiria pesa zake ikianza kumjaa kwa maana aliahidi kuhakikisha kwamba ata mshuhulikia mtu huyo aliye chukua pesa hizo siku atakayo mfahamu



‘Una uhakika Julieth”

ndio baba nina uhakika wa asilimia mia moja na habari nyingine ambayo sio nzuri kwetu. Josephine amekuwa ndio chief staff wa hapa ikulu kwa hiyo hata mimi nipo chini yake’

‘Nini?’

‘Ndio Josephine ni bosi wangu hapa ikulu hivyo ina bidi kuwa makini sana kwenye mipango yetu’

Julieth aliendelea kumuhabarisha baba yake kwa meseji hizo huku kila meseji ambayo ana ituma, akisha hakikisha kwamba ime somwa ana ifuta ili kuficha kinacho endelea endapo pale tu mume wake ata ishika simu yake.

Nabiii Sanga akashusha pumzi huku akitazama picha hiyo. Akawatazama watuu walio kusanyika hapo nyumbani kwake kwa ajili ya kuhuduria misiba ya watoto wake pamoja na ndugu zake ambao walifariki kwenye hoteli iliyo shambuliwa na bomu.

“Habari mtumishi”

Mzee mmoja alimsalimia kwa heshima.

“Salama mtumishi. Habari ya wewe”

“Mungu ana tupigania. Pole sana kwa misiba iliyo tokea”

“Nimesha poa”

“Taratibu za kuzika zipo vipi?”

“Aahh tuta watangazia”

“Sawa mtumishi”

Nabii Sanga akaachana na mzee huyo, akamuita mke wake kwa ishara ambaye ana zungumza na baadhi ya wamama wezake walio fika nyumbani hapo kumpa pole. Moja kwa moja wakaelekea chumbani kwao.

“Mke wangu una kumbuka ile siku tuliyo kutana na yule mtu wa kutisha?”

“Kwa nini nisiikumbuke wakati ile siku ndio ilianzisha mikosi hii yote”

“Una weza kufirikia ni nani ambaye ana weza kuwa muhisika?”

“Mmmm sijui kwani ume mpata muhusika?”

“Ndio”

“Ni nani?”

“Angalia hii picha”

Mrs Sanga akaitazama picha hiyo na kujikuta akishangaa.

“Hapa si ikulu”

“Ndio na huyo ni Magreth”

“Magreth gani?”

“Magreth huyu huyu anaye tutatiza vichwa vyetu”

“Ilikuwaje akawa na sauti mbaya kama ile?”

“Hata sifahamu na hapa Julieth ndio amenitumia hiyo picha na isitoshe ameniambia kwamba Josephine amekuwa ni chief staff wa ikulu hivyo, Josephine ana cheo kikubwa kuliko na Julieth.”

“Mmmm mume wangu hembu tuyaache hayo mambo. Tuwapumzishe kwanza watoto wetu, tukisha maliza ndio tuwafikirie hao wapumbavu”

“Sawa mke wangu ila ile pesa yangu ina niuma?”

“Kwa hiyo pesa ni muhimu kuliko wanao au?”

Mrs Sanga aliuliza kwa sauti iliyo jaa machungu mengi sana na kumfanya nabii Sanga kukaa kimya huku akimtazama mke wake ambaye ana jitahidi kuwa katika hali ya kawaida, ila ukweli ni kwamba ana pitia kipindi kigumu sana kwenye maisha yake.

***

Josephine na Magreth wakafika katika hospitali ya Muhimbili. Moja kwa moja wakaelekea katika chumba cha kuhifadhia maiti.

“Una weza kuingia?”

Magreth alimuuliza Josephine huku akimtazama usoni mwake kwa maana sio jambo rahisi kwa mwanamke kuingia kwenye chumba kama hicho.

“Ndio”

Josephine alijubu kwa ujasiri, wakaongozana na daktari na moja kwa moja akawapelekea kadi kadika friji alilo hifadhiwa Juma. Daktari akavuta mwili wa Juma nje na wakaanza kuutazama, Magreth machozi yakanza kumlenga lenga huku akiajiapiza kwamba ni lazima ata muua Evans kwa maana yeye ndio chanzo cha kifo cha Juma. Josephine hakutokwa na chozi lolote zaidi ya kuendelea kumchukuru Mungu kwa kila jambo. Walipo maliza kuangalia mwili wa Juma, wakatoka ndani hapo.

“Lazima nimuue Evans”

Magreth alizungumza huku akiwa amejawa na jazba kubwa sana. Josephine hakuzungumza jambo lolote, wakaingia kwenye gari na kuanza safari ya kuelekea nyumbani.

“Ndugu wa Juma una wafahamu?”

Josephine alizungmza kwa sauti ya upole huku akimtazama Magreth usoni mwake.

“Siwafahamu. Labda tuangalie namba kwenye simu yake.”

Wakafikishwa nyumbani na dereva ambaye emepewa jukumu la kumuendesha Josephine kwenye mizunguko yake yote. Wakaichukua simu ya Juma na kuanza kuipekua pekua, wakakuta namba iliyo andikwa jina la My Dady. Magreth akaipiga namba hiyo na kwa bahati akaikuta ipo hewani, simu hiyo ikaanza kuita na baada ya sekunde kumi ikapokelewa.

“Habari yako”

Magreth alianza kuzungumza.

“Ahaa salama. Nani wewe unaye tumia simu ya kijana wangu”

“Nina itwa Magreth ni bosi wa Juma”

“Ohoo habari yako binti”

“Salama mzee wangu. Upo wapi kwa sasa?”

“Nina toka shambani nina elekea nyumbani. Vipi kwema?”

“Ahaa mzee wangu nina kuomba ukifika nyumbani uweze kunipigia kwenye hii namba ya Juma”

“Mmmm kwa nini, vipi binti kuna tatizo lililo jitokeza?”

“Tafadhali mzee wangu nina kuomba sana ukifika uweze kuwasiliana na mimi”

“Una niogopesha binti”

“Hapana na hivi una patikana mkoa gani?”

“Tanga, Handeni”

“Sawa basi nina kuomba ukifika unipigie”

“Sawa binti”

Magreth akakata simu kwa maana hakuhitaji kumueleza mzee huyo bahari ya kifo cha Juma hadi pale atakapofika nyumbani kwake. Baada ya dakika kumi simu ya Juma ikaanza kuita, Magreth akaitazama kwa sekunde kadha akisha akaipokea.

“Haloo”

“Ndio mzee”

“Nimesha fika nyumbani binti yangu. Ehee niambie kwema huko”

“Sio kwema mzee wangu”

“Mmmmm kuna nini tena?”

“Usiku wa kuamkia jana kuna shambulizi la majambazi lilitokea kwa bahati mbaya Juma alipigwa risasi”

“NINI……!!!”

Mzee huyo alihamaki na kumfanya Magreth kujishauri kwa sekunde kadha kumueleza juu ya taarifa hiyo ambayo sio nzuri kabisa kwa mzazi hususani yule ambaye mategemeo yake yote ameyaweka kwa mwanaye.

“Ndio mzee wangu”

“Niambie hali yake vipi?”

“Sio nzuri mzee, nina kuomba uweze kuja Dar es Salaam kama ita wezekana”

“Sawa nina jiandaa sasa hivi nina kuja”

Simu ikakatwa na kumfanya Magreth kumtazama Josephine aliye jikunyata kwenye sofa huku akiendelea kuvuta kumbukumbu za uwepo wa Juma ndani hapo. Josephine akanyanyuka na kuingia katika chumba alicho kuwa ana lala na Juma. Akachukua moja ya tisheti yake na kuikumbatia. Ujasiri ambao alijitahidi kuutengeneza ukamuishia kabisa na kujikuta akianza kulia kwa uchungu sana. Kilio cha Josephine kiliyafikia vizuri masikio ya Magreth ambaye ame kaa sebleni.

Taratibu Magreth akatoka ndani hapo. Akasimama eneo lililo tapakaa damu za Juma ambazo kwa muda huo zimesha kauka.

‘Evans kwa nini umefikia huku? Kwa nini malipo yako una hitaji kuwapatia wasio na haki na ambao hawajahusika kwenye chochote kwenye mtafaruku wetu?’

Magreth alizungumza kwa sauti ya upole huku akizitazama damu hizo zilizo chora alama ya kuburuzwa hadi kwenye maua. Simu ya Juma ikaanza kuita na Magreth akaitazama kwa sekunde kadhaa kisha akaipokea.

“Sasa binti, nimesha pata gari. Niambie yupo hospitali gani?”

“Muhimbili mzee”

“Nina mpatia namba mjomba wake naye yupo hapo Dar ata kupigia ili aweze kufika hapo kabla yangu”

“Sawa mzee”

Magreth akarudi ndani, kabla ya kuingia chumbani kwa Julieth simu ya Juma ikaanza kuingia, akaitazama namba hiyo ngeni kisha akaipokea.

“Haloo”

“Nime pewa namba na shemeji yangu, amenieleza hali ya Juma vipi upo Muhimbili wodi gani?”

“Upo wapi kwa sasa?”

“Nipo kwenye bodaboda”

“Sasa nina kuomba tukutane hapo Muhimbili”

“Sawa”

Magreth akapitiliza hadi chumbani kwa Jossephine na kumkuta akiwa amejilaza kitandani huku machozi yakimbubuika.

“Jose nina kwenda muhimbili kuonana na mjomba wa Juma”

“Tuna kwenda wote”

Josephine alizungumza huku akipangusa machozi usoni mwake. Wakaondoka nyumbani hapo na kuelekea Muhimbili, wakakutana na mjomba wa Juma ambaye kiumri kidogo hawajapisha na Juma.

“Mjomba wangu yupo wadi gani?”

Jamaa huyo aliuliza kwa shahuku kubwa.

“Hadi tunavyo zungumza hivi sasa Juma amesha fariki duniani”

Magreth alizungumza kwa kujiamini na kujikaza kwa hali ya juu. Jaama huyo macho yakamtoka, akatamani kuzungumza jambo ila mdomo wake ukashindwa kabisa kuzungumza. Josephine naye machozi yakaendelea kumbubujika kwani katika kipindi hicho ni kigumu sana.

“Mj…omba wangu ame kufa?”

“Ndio”

“Oohoo Mungu ni nini sasa hii”

Jamaa alilalama ila malalamiko yake kwa Mungu hayawezi kubadilisha chochote kwa maana hakuna ambaye anaweza kutengua maamuzi ya Mungu juu ya mtu ambaye tayari amesha fariki duania. Wakaka hospitalini hapo hadi baba yake Juma alipo fika. Naye alipo zipata habari za kijana wake tegemezi kwenye familia yake alihisi kuchanganyikiwa, alizungumza maneno ya kila ina ambayo mengi ya hayo hayakuwa na maana wala tija ya aina yoyote. Taratibu za kuusafirisha mwiliw a Juma kulelekea mkoani Tanga handeni zikaanza. Raisi Mtenzi akaamuru gari maalumu ya kubebea maiti kuhakikisha kwamba wana usafirisha mwili wa Juma hadi kijijini kwao.

“Niwatakie safari njema”

“Tuna shukuru muheshimiwa”

Magreth alizungumza huku wakiwa wana zungumza na raisi Mtenzi kwa kupitia video call. Wakasha gari lao na kujumuika na familia ya Juma, wafanyakazi wa mgahawa na marafiki zake wa karibu katika safari hiyo ya kuelekea kijijini kwao.

Ndani ya gari lake Magreth yupo na Josephine pamoja na wafanyakazi wengine watatu huku wengine wakiwa wamepanda kwenye gari zilizopo nyuma. Kifo cha Juma kila mtu alihisi ni kama filamu isiyo isha, hapakuwa na aliye amini, hususani Magreth ambaye alimsihi sana Juma kuhakikisha kwamba ana funga geti na hamruhusu mtu wa aina yoyote kuingia ndani hapo.

Majira ya saa tisa usiku wakafika katika mji wa Kwamsisi. Moja kwa moja wakaeleka katika nyumba ya Mzee Sanze ambaye ndio baba yake Juma. Umati wa watu walio kusanyika hapo kwa kweli, Josephine na Magreth hawakuamini kama wata kuta watu wengi kiasi hicho. Vilio vilirindima kwa wanamama walio kusanyika eneo hilo.

“Usije uka sema kwamba ulikuwa na mahusiano ya kimapenzi na Juma”

Magreth alimsisitizia Josephine.

“Sawa”

“Jambo jengine hakikisha una kuwa karibu nami kila wakati, huku ni kijijini, hatujui ni nini kitakacho kwenda kutokea”

“Sawa”

Wakakaribishwa na wana familia walipo eneo hilo. Hapakuwa na hata mtu mmoja aliye pata lepe la usingizi hadi pana pambazuka. Taratibu zote za mazishi ya kiislamu zika fanyika na ilipo fika majira ya saa nne asubuhi, wanaume wakelekea makaburini na kuupumzisha mwili wa Juma.

“Juma alikuwa ndio tegemezi langu hapa nyumbani”

Baba Juma alizugumza na Magreth mara baada ya kutoka makaburini.

“Juma alikuwa ana nijengea hiyo nyumba yangu hapo juu, ila haijaisha na Mungu ameamua kumchukua”

Magreth akaitazama nyumba hiyo ambayo ipo katika kiwango cha madirisha.

“Ila mwanangu siku zote amekuwa akikusifia kwamba ana bosi mzuri. Hakika nime weza kuona jinsi ulivyo jitoa hadi mwili wa mwanangu ulipo fika hapa”

“Usijali mzee wangu, kila kitu Mungu ndio anaye panga. Ila nikuhakikishie kwamba nita zitimiza ndoto za Juma. Hiyo nyumba hapo nita ijenga yote hadi iishe”

“Ohoo asante Mungu mwanangu”

“Pia nita hakikisha tuna mpata aliye husika na shambulizi la Juma na nita hakikishaa na lipa kwa kile alicho kifanya”

“Nina shukuru sana binti yangu”

Josephine akafika eneo hilo walipo simama baba Juma pamoja na Magreth.

“Baba huyu ana itwa Josephine ni ndugu yangu, tulishindwa kutambulishana kutokana na hali ilivyo kuwa”

“Ni kweli, karibu sana Josephine, ila jina lako sio ngeni sana masikoni mwangu”

“Asante baba”

“Juma alisha wahi kuniambia kwamba ana msichana aliye mpata ana itwa Josephine je ni wewe?”

Magreth na Josephine wakatazamana.

“Ndio baba ni mimi”

“Ohooo pole sana mwanangu, natambua na wewe una pitia kipindi kigumu”

“Nashukuru baba.”

Josephine alizungumza kwa sauti ya masikitiko huku akimtazama baba Juma.

“Natambua wewe ni binti mdogo na mulikuwa na melengo mengi sana na mwezako ila Mungu ameamua kuzikatisha ndoto zenu. Mimi nina kupa baraka zote za maisha yako ya mbeleni huko una weza kutafuta mchumba wa kukuoa”

“Asante sana baba”

Magreth, Josephine pamoja na wafanyakazi wa Magreth wakaka nyumbani hapo kwa siku mbili kisha wakarudi jijini Dar es Salam huku Magreth akiwa amesha toa nusu ya kiasi cha pesa cha kuijenga nyumba ya baba Juma.

***

Siku ya mazishi ya watoto wa nabii Sanga pamoja na wana familia wengine ikawadia. Watu wengi kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya Tanzania wakakusanyika katika makaburi kuhushudia mazishi hayo ambayo kwa kweli yame iumiza sana familia ya nabii Sanga. Raisi Mtenzi naye ame hudhuria kwenye mazishi hayo.

Ulinzi ulizidi kuimarishwa kile eneo la makaburi kwani hawahitaji makosa yaliyo tokea awali kutokea tena. Magreth na Josephine nao waliweza kuungana na wana familia kwenye shuhuli hiyo.

Macho ya Zuma aliye jitengenezea sura ya kizee pamoja na kujibandika ndevu za bandika kuhakikisha kwamba hajulikani na mtu yoyote, nayo yakaanza kazi ya kupeleleza eneo walilo kaa wana familia na akafanikiwa kuwaona Julieth na Jery ambao nao wapo kwenye listi ya watu ambao ana hitaji kuwaua. Jambo jengine lilizo zidi kumfurahisha Zuma ni uwepo wa Josephine pamoja na Magreth kwenye msiba huo.

‘Leo hakuna hata mmoja wenua mbaye nita muacha hai. Lazima wote mufe’

Zuma alizungumza kimoyo moyo huku akiwatazama Josephine, Magreth. Kisha macho yake akayahamishia kwa Jery na Juluetha ambao wameshikana mikono huku wakiendelea kusikiliza sala hiyo ya mazishi inayo endelea hivi sasa.



“Mage”

Josephine alimuita Magreth kwa sauti ya kunong’oneza.

“Mmmm”

“Yule muuaji yupo hapa”

“Ehhee!!”

Magreth alishangaa kidogo huku akianza kuangaza angaza macho kwanye makundi ya watu walipo hapo makaburini.

“Yupo wapi?”

“Yule pale”

Josephine alimuonyesha Magret kwa ishara ya macho tu ili kuto mstua Zuma ambaye ana wakazia macho Jery na Julieth.

“Yule mzee pale?”

“Ndio, roho wa Mungu ana nionyesha ndio yule”

“Wewe baki hapa”

“Una kwenda sasa hivi kumkamata?”

“Ndio”

“Hapana acha kwanza ibada iishe, ila kuwa naye makini usimuache aondoke.”

“Sawa ila mbona ana mtazama sana Jery na Julieth”

“Nao wapo kwenye mpango wa Evans kuwaua”

“Mungu wangu huyo Evans amechanganyikiwa au?”

“Sijajua ila ndio mpango wake”

“Sawa wewe baki hapa acha nijifanye nina zuga kwa kuzungumza na simu”

“Poa”

Magretha akanyanyuka kwenye kiti alicho kalia, akaondoa eneo hilo huku akijifanya akiminya minya simu yake na kuiweka sikioni mwake. Zuma akamuona Magreth akielekea eneo la magesho ya magari.

‘Hii ndio nafasi’

Zuma alizungumza kimoyo moyo na kuanza kueleeka eneo anapo kwenye Magreth pasipo kutambua kwamba huo ni mtego na mtu ambaye ana mfwata sio wa kawaida kama anavyo muona. Magreth akasimama pembeni ya gari lake ambalo lipo katikati ya magari ya watu wengine walio udhuria mazishi hayo a kifahari. Zuma akafika kaaribu na eneo hilo la gari la Magreth, akachomua bastola yake kiunoni ambayo ameifunga kiwambo cha kuzuia sauti. Akajibanza kwenye gari la nyuma ya gari la Magreth. Magreth kutokana naye ana mtega Zuma aliweza kuona kila hatua anayo ifanya. Magreth akajifanya ana fungua mlango wa gari lake na kumfanya Zuma kuanza kumfwata kwa kasi huku bastola yake akiwa ameielekezea chini. Kitendo cha kufika hatua tatu kutoka eneo ambalo Magreth amesimama huku akiwa amempa mgongo. Magreth akageuka kwa kasi ya ajabu huku akijituma hewani na kufyatua teke kwa mguu wake wa kulia, ambalo moja kwa moja likatua kifuani mwa Zuma na kumuagusha chini huku bastola yake ikiangukia chini ya moja ya gari lililopo pembeni. Zuma akajawa na mshangao jinsi shambulizi hilo lilivyo mpata kwa maana sifa za watu alio pewa ni kwamba ni watu wa kawaida ambao hawana uwezo wowote.

Magreth hakutaka kumpa nafasi yoyote Zuma ya kunyanyuka au kujipanga kwenye mashambulizi yake kwa maana hamjui ni mtu wa aina gani. Magreth akanyanyua juu mguu wake wa kulia na lengo lake kubwa ni utua katika sehemu za siri za Zuma. Zuma kwa haraka akabingirikika pembeni na kiatu hicho cha Magreth chenye kisigino kirefu kidogo kika tua chini. Zuma kwa haraka akanyanyuka na kuanza kurusha makombora ya ngumi nzito nzito ambazo Magreth alijitahidi kuzikwepa. Zuma akarusha teke amabalo, Magreth alilikwepa na likapiga kwenye moja ya gari la pembeni hadi likasababisha kioo cha pembeni cha gari hilo kupasuka.

“Shitii”

Magreth alishangaa nguvu alizo kuwa nazo mtu huyo na kumfanya azidi kuwa makini kwa maana endapo ata pigwa na ngumi au teke la Zuma basi ni lazima atakuwa katika hali mbaya. Magreth akaanza kutumia mapigo ya taekwondo ambayo sifa yake ni kwamba yana tumia nguvu na nitagari pale yanapo mpata mpigwaji.

Mateke mawili mfululizo aliyo tapiga Magreth, Zuma alikwepa moja ila moja likampata shigoni mwake na kumtumbisha na kumfanya ahisi kizunguzungu. Magreth akaanza kuufahamu udhaifu wa Zuma, ana onekana ni mtumiaji wa nguvu sana na nimzito kwenye kutumia mwili wake.

Magreth akaelendelea kushasha mateke mfululizo, amgayo mengi Zuma aliweza kuyazuia kwa mikono yake huku akirudi nyuma nyuma. Kujilinda kwa Zuma, ina mpa nafasi nzuri ya kumsoma Magreth ambaye ana onekana kuwa ni mwiba kwake.

Magrhet akaruka staili iitwayo ‘flaying twin foot side kick’ ambayo, miguu yake yote miwili ilitua kifuani mwa Zuma na kumfanya arushwe na ujibamiza kwenye moja ya gari lilitegwa alarm na likaanza kupiga kelele zilizo wafanya askari walipo eneo hilo kuanza kukimbilia eneo hilo. Zuma akataka kunyanyuka ila akashindwa na kujikuta akitema damu kwa maana mateke hayo yaliweza kuvunja mbavu za kifuani mwake.

Askari hadi wanafika eneohilo wakamkuta Magreth akiwa amekunja ngumi huku jasho likimwagika usoni mwake huku Zuma akiwa amejigemeza kwenye gari na damu zikimchuruzika mdomoni mwake.

“Mkamateni huyo ni jambazi’

Magreth alizungumza huku akimnyooshea mkono Zuma.

“Wewe ni nani kwani?”

Askari mmoja aliuliza huku akimtazama Magreth usoni mwake.

“Kamuulize raisi wako mimi ni nani, mpigeni pingu”

Askari hao wanne wakaishiwa pozi na wakaanza kumpapasa Zuma na walipo hakikisha hana silaha yoyote, wakamfunga pingu. Magreth akamsogelea Zuma, akabandua ndevu hizo za bandia pamoja na sura hiyo ya bandia na kuwafanya askari hao kujawa na mshangao kwa maana walihisi mtu huyo ata kuwa ni mzee.

“Uta lipa kwa kifo cha Juma”

“Hahaha….aha.a….”

Zuma alicheka kwa dharau huku akimtazama Magreth.

“Kunikamata mimi sio mwishowa kufa kwenu”

“Hembu musimpeleke popote”

Magreth alizungumza huku akimtoa simu yake mfukoni, kwa bahati nzuri akaikuta ikiwa haijavunjika. Akamtumia Josephine meseji.

‘Nimemkamata muuaji wa Juma’

‘Kweli?’

‘Ndio nipo naye hapa. Mapatie taarifa raisi ili anipe maelekezo ya nini nifanye’

‘Sawa’

Josephine akamsogelea raisi Mtenzi sehemu alipo kaa.

“Muheshimiwa Magreth amafanikiwa kumkamata muuaji wa Juma na alikuwa yupo kwenye mpango wa kutuua sisi pamoja na Jery na mke wake”

Josephine alizungumza kwa kunong’oneza na kumfanya raisi Mtenzi kustuka kidogo.

“Yupo wapi?”

“Ngoja nimtumie ujumbe ila nina hisi wapo hapa hapa makaburini”

“Hembu mpigie simu”

Josephine akampigia simu Magreth.

“Vipi?”

“Nipe nizungumze naye”

Josephine akampatia raisi Mtenzi simu hiyo.

“Mage nilichoa ambiwa ni kweli?”

“Ndio muheshimiwa”

“Upo na nani?”

“Nipo na askari wanne hapa pamoja na muhalifu”

“Nina mtuma mkuu wa jeshi ana kuja na vijana wake hapo muta mkabidhi huyo mshenzi”

“Sawa muheshimiwa raisi”

Raisi Mtenzi alizungumza kwa sauti ya chini chini. Akakata simu na kumrudishia Josephine simu yake. Raisi mtenzi akamuita jenerali wa jeshi kwa ishara na akamfwata hapo.

“Kuna muhalifu wa aliye kwua amepanga kuwaua wanangu, amekamatwa nenda na chief sstaff wangu kwenye eneo alipo kamatwa hakikisha ana wekwa chini ya ulinzi”

“Sawa mkuu”

Josephine na jenerali huyo wa jeshi wakaondoka eneo hilo na kumfika eneo la magesho ya magari. Wakamkuta Zuma akiwa hoi bin taabani.

“Shuhuli hiyo ameifanya nani?”

Jenerali wajeshi aliuliza.

“Ni mimi”

“Magreth alizungumza kwa kujiamini na kumfanya jenerali wa jeshi kujawa na mshangao kwa maana alikuwa akizisikia tua sifa za Magreth ila hakuwahi kukutaa naye uso kwa uso.

“Kazi nzuri”

“Shukrani”

Ulinzi wa Zuma ukazidi kuongezeka, wanajeshi wakachukua jukumu la kumuweka kizuizini huku wakisurbiria maamuzi ya raisi.

“Ume umia?”

Josephine alimuuliza Magreth ambaye ana onekana kujawa na hasira dhidi ya Zuma.

“Hapana”

Magreth akaondoka hapo na kuingia kwenye gari lake kwa maana ana hisi kuka kwake hapo kuna weza kumfanya akafanya maamuzi mabaya ya kumuua jamaa huyo. Mazishi yalipo kwisha wakaondoka makaburini huku njia nzima Magreth akiwa kimya sana. Zuma moja kwa moja akapelekwa makao makuu ya kitengo cha NSA na akafungiwa katika chumba maalumu cha mahojiano. Magreth na Josephine wakafika ikulu na moja kwa moja wakaelekea katika ofisi ya Josephine.

“Nahitaji kumuhoji yule jamaa”

Magreth alizungumza huku akizunguka zunguka ndani ya ofisi hiyo.

“Ila kumbuka wewe sio mtumishi wa serikali”

“Natambua ila mimi ndio nime mkamata na kama kumuua basi ninge amua kumuua mimi mwenyewe”

Josephine akashusha pumzi huku akimtazama Magreth usoni mwake jinsi anavyo hema kwa hasira sana.

“Mage hili swala tuliwaachie vyombo ya ulinzi na usalama. Wao ndio watatuambia ni wapi walipo fikia”

“No nahitaji kumaliza hili jambo”

“Kivipi?”

“Nina hitaji kumshuhulikia Evans mimi mwenyewe”

“Mmmmm!! Sawa”

Josephine alizungumza kwa sauti ya upole kwa maana Magreth ana onekana kudhamiria kufanya hilo analo hitaji kulifanya.

***

Msafara wa raisi Mtenzi ukasimama katika makao makuu ya kitengo cha NSA. Raisi Mtenzi akashuka kwenye gari lake huku walinzi wake wakiendelea kuimarisha ulinzi. Moja kwa moja wakaelekea katika ofisi za mzee Mbogo na akapolekewa vizuri.

“Nahitaji kumuona mtuhimiwa aliye kamatwa na Magreth”

“Sawa muheshimiwa kwa sasa ana patiwa huduma kwa maana eneo la kifuani kuna mbavu zime vunjika”

“Ina maana alipiwa sana?”

“Yaa alipigika yule binti sio mtu wa kimchezo mchezo”

Mzee Mbogo alizungumza huku akiwa amejawa na furaha. Baada ya Zuma kupewa matibabu, akaingizwa kwenye chumba cha mahojiano.

“Muheshimiwa maandalizi tayari”

Msaidii wa Mzee Mbogo alizungumza. Raisi Mtenzi na mzee Mbogo wakaelekea katika chumba hicho. Kabla hawajaingia ndani raisi Mtenzi akavua koti lake la suti na kumkabidhi mlinzi wake.

“Nahitaji kuingia peke yangu na kamera zote pamoja na vivaa vya kurekodi vizimwe”

“Sawa muheshimiwa”

Raisi Mtenzi mara baada ya kutoa agizo hilo akaingia ndani hapo. Katika chumba cha apande wa pili cha mahojiano, akabaki mzee Mbogo pamoja na mlinzi namba moja wa raisi Mtenzi. Wafanyakazi wa chumba hicho wanao dili na maswala ya kurekodi, wakatoka nje. Raisi Mtenzi akavuta kiti cha pembeni huku akimtazama Zuma usoni mwake ambaye alionekana kustuka kidogo.

“Huyu ni wewe”

Raisi Mtenzi alizungumza huku akimuonyesha Zuma video ya CCTV kamera ilio mrekodi akiwa getini mwa Magreth na kumuua Juma.

“Ulihisi kwamba hato kukamata mara baada ya kupanga kumuua mwanangu Jery, mkwe wangu Julieth. Magreth na Josephine”

Zuma akastuka kidogo kwa maana swala hilo lilikuwa nis iri ya watu watutu ambao ni yeye, bosi wake na Evans ambaye ndio ame leta dili hilo.

“Zuma nina tambua kwamba muna conection na kundi la Al-Shabab. So nahitaji unipe muongozo wa wapi walipo Al-Shabab”

“Fuc** you”

Zuma alimtukana raisi Mtenzi na kumfanya atabasamu kidogo. Raisi Metnzi akanja vizuzir mikono ya shati lake.

“Hilo tusi mara ya mwisho kutukanwa ni kipindi nipo mazoezini tena depo ya polisi. Leo hii ume nitukana wewe king’ago. Hahaaa nilikuuliza kiwema sana, ila nina kuona kwamba huna ushirikiano mzuri kwangu”

Raisi Mtenzi akaisogeze meza hiyo iluyo watenganisha kati yake na Zuma akampiga teke la kifuani na kumfanya anguke kwa nyuma na kiti cheka. Zuma alipiga yowe la maumivu makali kwa maana kama ni mbavu zake ambazo kidogo lizisha anaza kutulia maumivu basi maumivu yame tibuka upya na mbaya zaidi ni kwamba hana uwezo wa kufanya jambo lolote kwani mikono yake pamoja miguu yake ime fungwa na pingu. Raisi Mtenzi bila ya huruma akamkanyaga kwa nguvu Zuma kifuani mwake na kuanza kukisaga saga kifua cha Zuma na kuzidi kumpatia maumivu makali hadi akaanza kutapika damu.

“Muheshimiwa ana weza akamuua”

Mlinziwa raisi Mtenzi alizungumza huku akiwa katika upande wa pili wa chumba hicho ambapo wame tenganishwa na kioo kizito na kigumu ambacho sio rahisi kwa mtu aliye chumba cha mahojiano kuona katika upande walipo mzee Mbogo na mlinzi huyo aliye jawa na wasiwasi mwingi sana kwa maana hakuwahi kumuona raisi akiwa katika hali ya hasira kama hiyo.



“Tulia kwanza”

Mzee Mboga alizungumza huku akimzuia mlinzi hiyo kwenda kumzuia raisi Mtenzi katika kumpatia adhabu hiyo kali Zuma.

“Zungumza Al-Shabab nita wapata wapi”

Raisi Mtenzi alizungumza kwa hasira sana huku akiendelea kumkandamiza Zuma kifuani mwake.

“Hahaaa kamtomb** mama yako”

Tusi hilo likawa kama limezifumua hasira za raisi Mtenzi kwa maana akaanza kumpiga Zuma mfululizo, kila sehemu ya mwili wake aliyo iona ina faa kwa kumpiga Zuma alifanya hivyo. Mzee Mbogo akaingia ndani hapo akiwa na mlinzi wa raisi.

“Musiniguse”

Raisi Mtenzi alizungumza huku akiwa amemkalia Zuma kiunoni mwake na akaendelea kumtandika ngumi mfululizo za usoni mwake.

“Muheshimiwa uta muua. Tuna mambo mengi sana ambayo tuna paswa kuyapata kutoka kwake”

Mzee Mbogo alizungumza huku wakimtazama jinsi raisi Mtenzi anavyo mshushia mangumi ya usoni Zuma na kuufanya uso wake kupasuka pasuka na kujaa damu nyingi.

Raisi Mtenzi akamuachia Zuma na akanyanyuka huku akiwa amejawa na hasira kali sana. Viganja vya mikono yake yote miwili vimejaa damu nyingi kwani ngumi hizo alizo mpiga Zuma ni nzito sana.

“Nahitaji apatiwe mateso hadi azungumze ukweli”

“Sawa muheshimiwa”

Raisi Mtenzi akatoka ndani hapo na moja kwa moja akaelekea bafuni kwa ajili ya kujisafisha. Mzee Mbogo akampigia simu daktari wa kitengo hicho na baada ya muda mfupi akafika eneo hilo.

“Ohoo Mungu wangu nini kilicho mpata”

“Mpime je ana weza kuachwa katika hali hiyo au ana paswa kupatiwa matibabu?”

“Kwa macho tu ya kawaida, huyu ana paswa kupatiwa matibabu muheshimiwa”

“Nahitaji mchome sindano ya maumivu?”

“Una maana gani muheshimiwa?”

“Nina hitaji uhakikishe kwamba ana chomwa sindano ya kumaptia maumivu makali kwa maana kuna maswali mahimu nahitaji kumuuliza”

“Ila muheshimiwa ana weza kufa”

“Nime kuambia mchome”

Mzee Mbogo alizungumza kwa msisitizo, dokta taratibu akafungua kibegi chake chenye sindao hizo maalimu za maumivu ambazo mara nyingi zina tumika kuwachoma wahalifu wabishi, na endapo uta chomwa sindano hiyo basi mwili mzima una patwa na maumivu ambayo yata kufanya uweze kuzungumza kila kitu. Mzee Mbogo akawaamru vijana wake kamnyanyua Zuma na wakamalisha kwenye kiti. Mikono ya Zuma ikafunga vizuri kwenye kiti hicho, kisha taratibu daktari akaanza kumchoma sindano hiyo. Muamivu katika mwili wa Zuma yakazidi kuongezeka mara dufu kwa maana sindano hiyo ni marasaba ya maumivu ya mtu anaye chomwa sindano ya kistapen.

“Al Shabab wapo wapi?”

Mzee Mbogo alimuuliza Zuma ambaye analia kama mtoto mdogo.

“Wapo Nigeria, wana fadhiliwa na Boko haramu”

Zuma alizungumza huku akilia kama mtoto mdogo.

“Una uhakika na unacho kizungumza?”

“Ndio, haki ya Mungu wapo nchini Nigeria na wamapewa hifadhi na Bokoharamu.”

Mzee Mbogo mara baada ya kupewa taarifa nyeti kama hiyo akamuamuru daktari kumchoma sindano ya usingizi Zuma na akarudisha kwenye chumba cha upasuaji.

“Muheshimiwa tume weza kupata data muimu”

Mzee Mbogo alizungumza huku akimtazama raisi Mtenzi anaye valia koti lake vizuri.

“Data gani?”

“Kundi la Al-Shabab kwa sasa lime jificha nchini Nigeria kwenye kambi za Bokoharamu”

“Ni lazima tulipe kwa kile walicho tufanyia. Anzeni kutafuta ni wapi zilipo kambi za Bokoharamu. Tumeelewana?”

“Ndio muheshimiwa tume elewana”

Raisi Mtenzi mara baada ya kuzungumza hivyo akaanza safari ya kurudi ikulu.

***

“Hei”

Jery alizungumza kwa sauti ya upole huku akimshika Julieth begani mwake mara baada ya kutoka bafuni kuoga.

“Niambie”

Josephine alizungumza kwa sauti ya kinyonge huku akijifunga kitambaa kichwani mwake kwa ajili ya kulala usiku huo.

“Niambie mume wangu”

“Una jisikiaje?”

“Nime choka kwa kweli, msiba umekuwa ni mzito sana kwa upande wetu. Kila kitu kinacho tokea kwa kweli nina hisi kama ni ndoto”

“Usijali mke wangu haya nimapito na kila jambo lita pita”

“Ila nita hakikisha hawa walio sababisha yaliyo tokea kwenye kwa ndugu zetu pamoja na wazazi wetu wana lipa”

Julieth alizungumza kwa msisitizo na kumfanya Jery kumtazama kwa sekunde kadhaa.

“Ahaa mke wangu, katika maisha yako epuka kitu kisasi”

“Una maana gani kuzungumza hivyo?”

“Endapo utakuwa ni mtu wa kulipa kisasi basi maisha yako yata kuwa ni yakulipiziwa visasi kwa maana hata yule unaye kwenda kumlipizia kisasi basi ata patikana msaizidi wake ambaye naye atahitaji kulipa kisasi kwa ajili ya yule uliye mtendea ubaya. Kiufupi tuyaache yapite, sawa mke wangu”

Jery alizungumza kwa sauti ya upole huku akimtazam Julieth usoni mwake.

“Sawa mume wangu”

Mlango wa chumba chao ukagongwa. Jery akanyanyuka taratibu na kuufungua.

“Shikamoo baba”

“Marahaba mume lala?”

“Hapana”

“Basi nina waomba sebleni”

Jery akaufunga mlango na kumtazama Julith aliye vaa gauni la kulalia. Julieth akajifunga tenge kisha wakatoka ndani hapo na kuelekea sebleni. Wakamtazama raisi Mtenzi ambaye uso wake una uoneka kutoa kuwa na furaha kabisa.

“Baba ume tuita”

Jery alizungumza kwa sauti ya upole huku akimtazama baba yake usoni.

“Muna mfahamu kijana anayye itwa Evabs?”

Julieth na Jery wakatazamana.

“Ndio baba”

“Kijana huyo aliweza kumtuma muuaji kwa ajili ya kuwaua”

Jery na Julieth waka stuka sana”

“Kwa nini?”

“Ina bidi nyinyi ndio niwaulize kwa nini?”

Julieth mapigo yake ya moyo yakaanza kumuenda kasi sana kwa maana katika familia hiyo ame weza kuwadanganya jambo moja kwamba yeye ni bikra na ukweli ni kwamba bikra yake ame itoa Evans huyo ambye wame mfanye wame mfanyia mambo mengi mabaya.

“Au ni kile kipindi ulicho tuma wale wapumbavu kwa ajili ya kumuu na wakashindwa?”

Raisi Mtenzi alimuuliza Jery na akajikuta akiendelea kukaa kimya.

“Sasa ule ujinga ambao uliifanya kipindi kile sasa matokeo yake ndio haya. Muna tambua kwamba leo makaburini ilikuwa ndio mwisho wenu?”

Jery na Julieth wakajikuta wakikaa vizuri kwenye sofa kwa maana hiyo nayo ni habari mpya kwao.

“Muuaji alikuja hadi makaburini ila muna paswa kumshukuru Magreth kwa maana yeye ndio aliye mkamta”

“Huyo muuaji ametokea wapi?”

Julieth aliuliza kwa sauti ya unyonge sana.

“Ni mmoja ya makomandoo ambao wana fanya kazi na kundi la Al-Shabab”

“Mungu wangu Al-Shabab tena?”

Jery alihamaki.

“Ndio hivyo. Sasa hatujui kuna watu wangapi ambo wame tumwa na huyo mshenzi Evans kuja kuwaua. Jambo la msingi hakikisheni kwamba muna kuwa makini. Hamtoi miguu yenu hapa ikulu pasipo utaratibu wa kuongozana na walinzi. Tumeelewana”

“Ndio baba”

“Usikumwema”

Raisi Mtenzi mara baada ya kuzungumza kanyanyuka na kuingia chumbani kwake na kuwaacha Jery na Julieth nao wakielekea chumbani kwao huku wakiwa wanyonge sana. Raisi Mtenzi akakitazama chumba chake kwa sekunde kadhaa, Kumbukumbu za mke wake, zikaanza kumjia kichwani mwake. Taratibu akaisogelea picha aliyo piga na mke wake, akaitazama kwa sekunde kadhaa na kujikuta machozi yakimwagika kwa maana mke wake ame muacha katika kipindi ambacho hakutaraji kabisa kwamba ata kufa.

“Huyu Evans ni mshenzi sana”

Jery alilama huku akizunguka zunguka ndani ya chumba hicho. Julieth hakzungumza kitu chochote zaidi ya kuwazia ni jinsi gani Evans yule aliye kuwa choka mbaya leo hii ana uwezo wa kumlipa komandoo wa kundi la Al-Shabab kwa ajili ya kuwaua.

‘Mmmm amezipatia wapi hizo pesa?’

“Mke wangu ume ona madhara ya kisasi haya. Tazama pale makaburi tulivyo kuwa tune jiachia kumbe tulikuwa tuma windwa roho zetu”

Julieth hakujibu chochote zaidi ya kuendelea kumtazama Jery anavyo haha kwa wasiwasi.

‘Hapa mume sina’

Julieth alizungumza kimoyo moyo kwa maana ameweza kuugundua udhaifu wa Jery ni mtu ambaye hana maamuzi magumu na nimuoga sana.

‘Sijui hata itakuwaje mke wangu”

“Jery kama amekamatwa huyo muuaji basi ata patikana na huyo Evans”

“Una hisi ni rahisi kiasi hicho mke wangu. Kama tulipunyuka kwenye mabomu ya kwanza, leo tume punyuka bas linalo fwata ni sisi kufa”

“Jery acha woga mume wangu. Ndio maana nime kuambi ni lazima tujilinde na kupambana, endapo tuta endelea kujifanya ni watakatifu tuta uwawa kama unavyo sema”

Julieth alizungumza kwa msisitizo na kumfanya Jery atingishe kichwa akiashiria kukubaliana na kile anacho kizungumza mke wake.

***

Taratibu Magreth akasimamisha gari lake katika geti kuu la kuingilia makao makuu ya kitengo cha NSA. Josephine akatoa kitambulisho chake na kumpatia mmoja wa askari walipo getini hapo. Askari huyo akasoma kitambulisho hicho.

“Nawe naomba”

“Huyu ni mlinzi wangu”

Josephine alitumia nafasi hiyo kumtambulisha Magretj kwa maana ana tambua kwamba hana kitambulisho chochote ambacho kina weza kumuwezesha kuingia katika kitengo hicho. Wakaruhusiwa kuingia ndani hapo.

“Hah anime kuwa mlinzi wako”

“Sasa ndugu yangu ninge kutambulishaje, nina imani kwamba wange kuzuia”

“Usijali nime kuelewa”

Magreth akasimamisha gari lake eneo la maegesho, wakashuka na moja kwa moja wakaelekea ofisini kwa mzee Mbogo.

“Karibuni nina ona mume nifanyia surprise”

“Yaa ni kweli ndugu yangu ana shindwa kupata usingizi hadi nika amua kumleta huku”

“Karibuni sana”

“Tuna shukuru”

“Kaeni”

“Asante”

“Ehee niambie ni nini kilicho waleta”

“Ahaa muheshimiwa kama unavyo tambua kosa alilo lifanya Juma kwetu. Ame tuondolea mpendwa wetu ame tuweka kwenye majonzi mengi sana Ila kuna jambo moja sana ambalo nina omba niweze kuliomba kwako”

Magreth alizungumza kwa sauti ya Upole kidogo.

“Ni kweli na pia hongera kwa kumkamata muhalifu”

“Nina shukuru, ila nafsi yangu haina furaha kumuona akiwa ana endelea kuishi. Tafadhali nina kuomba uweze kunipatia mtu huyo kama mume maliza kuzungumza naye. Nina hitaji kumuua kwa mkono wangu mimi mwenyewe”

“Mageeeee”

Josephine alilalama huku akimtaza Magreth kwa mshangao kwa maana kile alicho kuwa wamekipanga sicho hicho anacho kizungumza hapo.



Mzee Mbogoakamtazama Magreth usoni mwake kisha akamatzama na Josephine ambaye ana onekana kuwa ana pinga ombi hilo la Josephine.

“Tuta kupatia Zuma ili umuue”

“Mzee wangu nawe una kubaliana na hilo!!?”

Josephine aliuliza huku akiwa amejawa na mshangao mkubwa sana.

“Ndio nina kubaliana na hilo kwa maana watu kama Zuma hawana nafasi ya kuishi katika ulimwengu huu. Ila Magreth kuna kazi moja ambayo nina omba uweze kuifanya”

“Kazi gani?”

“Zuma ameweza kutupa muongozo kwamba sasa hivi Al-Shabab wana hifadhiwa na kundi la Bokoharamu lililopo nchini Nigeria. Ila kabla ya kufanya hivyo tuna hitaji kuweza kumpata muhisika wa hili shambulizi ambaye ni Evans. Je una weza kutusaidia katika hilo?”

“Ndio nina weza kufanya hivyo”

Magreth alijibu kwa kujiamini sana. Mzee Mbogo akatoa faili kwenye droo moja ya meza yake na kumkabidhi Magreth.

“Hilo ni faili linalo onyesha taarifa zote za Evans Shika. Kipindi alipo kuwa kijana mdogo aliweza kumuua baba yake mzazi”

Josephine alishangaa sana kusikia hivyo.

“Pia katika hii milipuko iliyo tokea yeye aliweza kufahamu kwamba ipo milipuko itakayo tokea na akanipatia na udhibitisho wa kwamba milipuko hiyo itatokea. Apo awali aliweza kuniambia kwamba yeye ni nabii na ana onyesha mambo hayo na Mungu na kweli milipuko ilipo tokea niliweza kumuamini kwa asilimia kadhaa japo sio nyingi. Alinieleza kwamba kiwango chake cha pesa alizo nazo amepata kutoka kwa Mungu na alinunua eneo kubwa Kigamboni kwa ajili ya kujenga kanisa na akauti yake ina kiwango kikubwa sana cha pesa za Kimarekani”

“Mmmm Evans kuwa nabii?”

“Ndio jinsi alivyo nieleza. Sikuhitaji kumfwatilia snaa kwa maana kwa kipindi hicho nilikuwa sifanyi kazi serikalini. Ila baada ya hili jambo lililo tokea nikaanza kuunganisha doti ambazo hapo awali sikuwahi kuziunganisha. Moja kwanza amemaliza chuo mwaka jana, hana kazi, hana biashara ina kuwaje ana kuwa na kiwango kikubwa cha pesa kama hicho. Hapo ndipo nikapata mashaka na kutambua kwamba msaada wote huuameupata kutoka kwenye kundi la kigaidi la Al-Shabab. Alijuaje Tanzania ita shambuliwa na mabomu? Nakumbuka niliweza kumpatia onyo la kuachana na Julieth kwamaana ni mpenzi wa mtoto wa raisi? Akalipo taka kuuwawa na Jery kipindi kile nina imani ndipo alipo weza kukutana na hao Al-Shabab na wakampatia msaada huo wote”

“Ngoja kwanza muheshimiwa. Ume sema Jery alitaka kumuua Evans?”

Josephine alimuuliza mzee Mbogo.

“Ndio alitaka kumuua mkoani Morogoro na aliweza kutuma kundi la wauaji ambao walishindwa kutekeleza adhima hiyo japo niliweza kumtuma kijana wangu mmoja kwa ajili ya kumlinda ila raisi aliweza kutoa oder ya Evans kukabidhiwa kwa wauaji hao”

Magreth macho yakamtoka kwa maana ana kumbuka siku hiyo yeye na Josephine walikuwa katika harakati za kumuokoa Evans na kwa bahati mbaya walipata ajali iliyo sababisha Josephine kuvunjika mguu.

“Raisi ndio alitoa oder ya Evans kuuwawa?”

“Ndio japo sikuhitaji iwe hivyo kwa maana niliweza kuona ni kijana mmoja ambaye yupo very smart na endapo ata kuwa katika serikali basi ana weza kumsaidia raisi”

“Kwa hiyo haya yote anayo yafanya Evans ni kutokana na raisin a mwanaye kuhitaji kumuua?”

Josephine aliuliza kwa sauti ya upole.

“Ndio”

“Ohoo Mungu wangu”

Josephine alihamaki huku akishusha pumzi.

“Mage, Mage Mage”

Mzee Mbogo aliita mara baadaya kumuona Magreth macho yakiwa yame mtoka huku akiwa anatazama sehemu moja ikiwa ni ishara ya kushikwa na bumbuwazi.

“Beee”

“Unawaza nini?”

“Hakuna mzee”

“Zungumza kama kuna jambo lina kusumbua kwa maana sihitaji kuwaficha jambo lolote kwenye hili swala kwa maana endapo hapo baadae kutatokea la kutokea basi nina uhakika muna weza kunichukia”

Josephine akamtazama Magreth anaye onekana kujawa sinto fahamu.

“Hei Mage upo sawa?”

“Ndio Jose”

“Magreth nina tambua kwamba ulikuwa na mahusiano na Evans na alikusaidia kupambana na vibaka siku ulipo kuwa una tembeza maandazi”

“Ulijuaje?”

“Mimi ni mpelelezi hivyo niliweza kuifwatilia historia ya Evans kipindi nilipo kuwa nina mshawishi kujiunga na NSA na niliweza kutambua chanzo cha nynyi kuachana ni pesa za nabii Sanga”

Magreth akashusha pumzi nyingi huku akikosa cha kuzungumza.

“Huwa katika hili nina amini kwamba Evans haya yote anayo yafanya ni kulipiza kisasi kwa nyinyi watu wanne mulio muumiza”

“Ila mimi sijamfanyia kosa?”

Josephine alijihami.

“Wewe kwenye hii listi haupo. Yupo Nabii Sanga, Magreth Jery na Julieth, na ipo siku nabii Sanga alimkamata kijana huyo kwa ajili ya wivu wake wa mapenzi kwako na kuhitaji kumuachanisha na binti yake Julieth”

“Ina tosha mzee sihitaji kusikiliza mambo ya nyuma”

Magreth alizungumza kwa msisitizo huku akionekana kuchukizwa na mazungumzo hayo.

“Mzee wangu niambie nini nifanye”

“Nahitaji Evans arudishwe nchini Tanzania na nita hitaji uhakikishe kwamba ana rudi akiwa hai, ukikamilisha hilo Zuma ni wako”

“Dili”

“Ndio dili”

Magreth na mzee Mbogo wakapeana mikono ikiwa ni ishara ya kukubaliana kwa utendaji wa kazi hiyo iliyopo mbele yao. Mzee Mbogo akafungua droo yake na kutoa kitambulisho cha Magreth

“Hicho ni kitambulicho chako, kinacho kuonyesha kwamba kuanzia hivi sasa uta kuwa ni mwana NSA”

Magreth akakisoma kitambulisho hicho ambacho kina picha yake.

“Nashukuru”

Magreth akakiweka kiweka mfukoni kitambulisho hicho.

“Ukiwa tayari kwa kwenda kuianza hiyo kazi ita bidi kuja ofisini kwangu na kupeana maelezo ya kuhakikisha kwamba tuna jua ni njia gani tuna pitia kwa ajili ya kuianza kazi hiyo.”

“Sawa, hili faili si nina paswa kwenda nalo?”

“Ndio, ila hakikisha huanzi kufanya kazi hiyo kabla ya kuwasiliana nasi”

“Sawa”

Magreth na Josephine wakatoka ofisini hapo na kuondoka makao makuu. Wakafika nyumbani wanapo ishi, Magreth hakuwa na furaha kabisa moyoni mwake, akajibwaga kwenye sofa na kuanza kulipekua upya faii hilo la Evans ambalo lina picha zake pamoja na picha za watu wenye ushirika naye wa sasa.

“Kumbe raisi naye ana mabalaa yake”

Josephine alizugumza huku akimtazama Magreth.

“Ndio una jua leo”

“Kwani nawe una tambua ubaya alio ufanya raisi?”

“Nauelewa kwamba tuna fanya kazi na mtu wa aina gani. Jambo la umakini kwako usijiachie sana kwake kwa maana muda wowote ana weza kubadilika na kutugeukia. Umenielewa?”

“Ndio”

Josephine alijibu kwa unyonge kwa maana kuba baadhi ya mambo ya siria ambayo Mungu bado hajamuonyesha juu ya raisi Mtenzi.

***

Mlango wa chumba cha Baby Al, ukagongwa. Akamtazama Evans aliye jilaza pembeni yake kwenye kitanda hicho cha tano kwa sita.

“Nani?”

“Ni mimi mkuu”

“Mbona usiku sana kuna nini?”

“Kuna habari mbaya”

“Nenda kawasikilize”

Evans alizungumza huku akimtomasa chuchu ya upande wa kulia ya Baby Al. Taratibu Baby Al akashuka kitandani, akavaa nguo zake na kufungua mlango huo. Mlinzi wake huyo akamkabidhi ipad inayo onyesha video ya Zuma akipigana na Magreth.

“Hii video ime weza kuwekwa kwenye mtandao wa Youtube usiku.”

Baby Al akastuka sana kuona jinsi Zuma anavyo pata kipigo kikali kutoka kwa mwanamke huyo ambaye ana mfahamu ni mmoja wa watu aliye tolewa oder ya kuuwawa. Mtu aliye rekodi video hiyo ana onekana yupo ndani ya gari la karibu na eneo la tukio hilo lilipo tokea.

Baby Al akarudi ndani na kumkabidhi Evans Ipad hiyo. Evans mara baada ya kuitazama kidogo kwa haraka akaka kitako kitandani huku macho yakiwa yame mtoka kwa maana Magreth anaye mjua sio huyo ambaye ana toa kipogo kama hicho kwa mwanaume mwenye miraba minne.

“Evans huyo ambaye ulitoa kazi ya kuuwawa ni nani?”

“Ni Magreth na ndio huyu”

“Huo uwezo wa kupigaana ameutolea wapi?”

“Hata mimi sifahamu”

“Hufahamu vipi ikiwa una muona mtu wangu ana pigwa kiasi hicho”

“Ila uliniambia kwmaba mtu wako ni Komandoo ila imekuwaje ana pigwa na mwanamke”

Baby Al akashusha pumzi huku akimtazama Evans.

“Hivi una hisi kumandoo ana weza kumpiga kila mtu”

“Hapo sawa, kwa maana uliniambia kwamba ana uwezo wa kujilinda ina kuwaje ana pigwa. Ona ona jinsi anavyo pigwa mateke”

“Acha kuitazama hiyo video na tuzungumze nini cha kufanya.”

Baby Al alizungumza huku akiwa amejawa na hasira kali sana. Evans akaiweka ipad hiyo pembeni na kumtazama Baby Al anaye hema kwa hasira kali.

“Kama Zuma ame kamatwa basi kuna asilimia kubwa sana ya huko tunapo kwenda hakutokuwa salama”

“Wapi kwani tuna kwenda?”

“Nigeria kwenye kambi ya Boko Haramu”

“Nini, Bokoharamu tena?”

“Ndio una shangaa nini?”

“Hapana ila Al-Shabab na Bokoharamu kuna uhusiano gani hapo?”

“Huu sio muda wa kujadiliana na maswali”

Mlango ukagongwa na kumfanya Baby Al kutembea kwa haraka hadi mlangoni hapo akaufungua na kumkuta mlinzi wake mwengine.

“Mzee ana hitaji kuzungumza na wewe”

Baby Al mapigo yake ya moyo yakaanza kumuenda kasi sana. Akaitazama simu hiyo anayo kabidhiwa na mlinzi wake. Akaichukua na kufunga mlango, akamuonyeshea Evans ishara ya kufunga kinywa chake na asizungumze neno lolote. Taratibu akaiweka simu hiyo sikioni mwake.

“Baba”

“Mbona simu yake haipatikani hewani?”

“Nina hisi ni network baba kwa maana tupo safarini”

“Una weza kuniambia ni kitu gani kilicho mrudisha Zuma nchini Tanzania?”

Swali la baba yake kidogo likamfanya Baby Al kukaa kimta huku akitafariki ni nini cha kumjibu baba yake huyo ambaye ni mkali sana.

“Ahaa baba Zuma kuna kazi alikuwa ana imalizia”

“Kazi gani?”

“Kuna watu alikwenda kuonana nao”

“Acha kunidanganya. Niambie ukweli ni nini kinacho endelea”

Baby Al akazidi kutetemeka kwa woga kwa maana ana mtambua vizuri kwamba baba yake sio mtu wa mchezo mchezo japo ana mapenzi mengi sana kwa binti yake ila hapendi upumbavu kabisa.

“Kuna watu alikwenda kuwaua na mmoja wao ni huyo aliye kuwa ana pigana naye”

“Pumbavu kweli wewe unamtumaje kwenye kazi ngumu kama hiyo?”

“Ahaa nina omba uni samehe baba”

“Sasa ondoka na helicopter na nina kuhitaji urudi nyumbani kwa maana kila kitu kita kuwa wazi ume nielewa”

“Ndio baba”

Simu ikakatwa na kumfanya Baby Al kuishiwa nguvu. Taratibu akaka kitandani huku akimtazama Evans ambaye ameshangazwa na hali hiyo.

“Ni nani huyo?”

“Baba yangu”

“Ana semaje”

“Ana hitaji nirudi nyumbani leo hii hii na niondoke na helicopter sasa sijui tuta ondokaje ikiwa sitaki kukuacha hapa peke yako kwa maana hawa watu wata kuua”

Baby Al alizungumza huku machozi yakimlenga lenga usoni mwake. Evans taratibu akamlanza Baby Al kifuani mwake.

“Hei baby”

“Mmmm”

“Una nipenda?”

“Ndio nakupenda Evans”

“Nakuomba unisaidie jambo moja”

“Jambo gani?”

“Nikutanishe na kiongozi wa kundi lolote la kigaidi ambalo una hisi kwamba wewe una wamudu. Nahitaji kuwa gaidi na nita hakisha nina kwenda kulipa kisasi kwa wale wote walio niumiza. Siwezi kulipa kisasi changu kwa kutumia pesa kwa maana wana kwenda kuingia matatizoni watu wasio jua chanzo cha hii vita. Tafadhali nisaidie katika hilo mpenzi wangu”

Evans alizungumza kwa msisitizo na hisi kali hadi Baby Al akajawa na mshangao kwa maana ina onyesha kwamba Evans ame dhamiria kabisa kufanya jambo hilo.



“Una taka kuwa gaidi?”

“Ndio nahitaji kuwa gaidi. Nahitaji kufanya haya mambo mimi peke yangu”

“Ila kabla sija kuunganisha nahitaji kukujua Evans. Wewe ni nani na kwa nini una taka kuyafanya haya yote peke yako”

Swali la Baby Al likamfanya Evans kukaa kimta kwa sekunde kadhaa huku akitafakari namna ya kumjibu mpenzi wake huyo mpya.

“Una ziona hizi alama mwilini mwangu?”

“Ndio alafu nilikuwa nina hitaji kukuuliza hayo makovu yote yame tokana na nini?”

“Hili ni kovu la kazwa na kubwa kuwepo katika mwili wangu. Kovu hili nilichomwa kisu nilipo kuwa nina mtetea msichana mmoja ambaye alikuwa ana uza maandazi kipindi hicho. Msichana huyu alibananishwa kwenye vichochoro na wavuta bangi au kwa jina jengine una weza kuwaita ni vibaka. Nakumbuka siku hiyo nilikuwa nina hama kutoka kwa mshkaji wangu na kujitafutia sehemu ya kupumzika. Kama mwanaume unavyo mkuta msichana mnyonge akiwa katika wakati mgumgu basi wengi wetu tuna jitahidi kuhakikisha kwmaba tuna msaidia. Niweza kupambana na wale vibaka ila kwa bahati mbaya mmoja wao alinichoma kisu cha hapa tumboni”

Evans alizungumza huku akimuonyesha Baby Al kovu hilo.

“Binti yule aliweza kunisaidia kwa kunikimbiza hospitali, aliweza kutafuta mfadhili wa kunilipia hayo matibabu hadi nikapona. Ila Yule binti alitokea kunipenda sana na mimi nilitokea kumpenda. Ila kumbe yule mfadhili wake alitokea kumpenda na akawa na mahusiano naye. Alimpatia kila kitu kuanzia nyumba, gari pesa na akamfungulia mradi mkubwa sana wa mgahawa”

Evans alizungumza kwa sauti ya upole na utaratibu huku kichwani mwake akiona matukio ya nyuma ya maisha yake jinsi yanavyo pita kama mkanda wa video.

“Yule msichana alinificha mambo yote hayo na nikawa nina shirikiana naye kwenye ile biashara yake kama mpenzi wangu. Sasa yule mtu wake aliweza kurudi na mimi nilikuwa nina muheshimu kama mchungaji mzuri na mwenye wito wa Mungu ndani yake. Kumbu ni mshenzi sana na mtu mwenye roho mbaya. Yule mzee aliweza kujnishikia bastola na kunitoa nyumbani kwa yule msichana na kuahidi kuniau pale tu atakapo nikuta nikiwa na mahusiano naye.”

“Huwezi amini niliondoka pale nyumbani nikiwa na nguo nilizo zivaa tu. Niliweza kukodi chumba kwenye hoteli na kwa bahati nzuri nikakutana na na msichana mmoja ambaye alitokea kunipenda na niliweza kubahatika kumtoa usichana wake. Binti huyu nilikuwa nina ishi naye kwenye hoteli hiyo na alikuwa na pesa za kutosha sana. Ila nilikuja kushangaa siku moja tulipo kamatwa na askari wa kitengo cha NSA. Hapo ndipo nilpo kuja kugundua kwamba yule msichana ni mtoto wa yule mzee aliye nishikia bastola na kuniachanisha na msichana nina mpenda. Msichana huyo naye na mbaya zaidi alikuwa na mahusiano ya muda mrefu na mtoto wa raisi ambaye ambaye alipo kuja kugundua kwamba mimi nina mahusiano na msichana wake, alituma kundi la majambazi ambao waliniteka na wakanipatia mateso ila niliweza kufanikiwa kuwatoroka majambazi hao.”

“Masikini mpenzi wangu pole sana. Sasa hao unao wazungumzia ni kina nani?”

“Yule msichana ambaye alikuwa ana uza maandazi ni huyo Magreth. Msichana ambaye alikuwa ni mpenzi wangu wa hotelini huyo Julieth na mwanaume wake ni Jery. Mzee aliye nitachukulia mwanamke niliye kuwa nina mpenda ni huyo nabii Sanga.”

Evans alizungumza huku akimuonyesha Baby Al picha za watu hao kwenye ipad aliyo ishika mkononi mwake.

“Yule binti mwengine ambaye ana itwa Josephine naye ame kufanya nini?”

“Yule binti ana maono ya kila jambo ambalo lina taka kwenda kutokea. Hivyo endapo tusipo muua huyo pia, basi ni ngumu sana kwa hawa watu wanne kuwapata kwenye tagert yangu ninayo ihitaji”

“Huo uwezo wake ame utolea wapi?”

“Ni Mungu ndio aliye mpatia hivyo ni lazima huyo afe alafu hawa wangine wafwate”

“Duuu sasa Zuma amesha kamatwa, sasa ita kuwaje?”

“Ndio maana nika kuomba sana kwamba nikutanishe au niungenishe na moja ya kundi la kigaidi. Nipate mafunzo nitakayo weza kudili mimi mwenyewe na hawa watu”

“Sinto kupelekea kwenye kundi la kigaidi ila kuna mtu ambye nita kukutanisha naye. Mtu huyo ni mara kumi na Zuma ana kila aina ya ujuzi katika maswala ya mapambano. Nina imani ana weza kukufundisha na ukawa mtu hatari sana, ila nina taka uniahidi jambo moja”

“Jambo gani?”

“Je uta kuwa na mimi hadi kufa?”

“Usijali nita kuwa nawe hadi kufa”

“Nashukuru tunza ahadi yako kwa maana ukienenda kinyume na ahadhi hiyo basi nita jua ni jinsi gani ambavyo nita dili na wewe.”

“Usijali mpenzi wangu usiwe na wasiwasi na mimi”

“Poa leo usiku tuta ondoka kuelekea nchini Russia, nita kuacha hivyo na mimi nita kwenda nchini Ufaransa”

“Sawa”

Evans alijbu huku akiwa ametawaliwa na furaha kubwa sana kwa maana ana amini kwamba sasa ata kwenda kupambana na maadui zake yeye mwenyewe.

***

“Mage Mage ona”

Josephine alizungumza huku akimkabidhi Magreth simu yake.

“Ni nini Jose”

“Tazama video yako hii nime tumiwa whatsapp na raisi”

“Video yangu ipi?”

Magreth kidogo alistuka na kucha kuandaa kifungua kinywa na kiuchukua simu hiyo ya Josephine. Akaanza kutazama jinsi anavyo pigana na Zuma. Akajawa na mshangao mkubwa sana kwa maana eneo lile kwa kumbukumbu zake ana kumbuka hapakuwa na mtu yoyote.

“Ni nani aliye irekodi hii video?”

“Sijajua ila ina onekana ni mtu ambaye alikuwa yupo ndani ya gari”

“Shiti hili tatizo”

“Tatizo gani ikiwa ime kuwa maarufu rafiki yangu”

“Jose tambua mimi ni mtu wa ina gani na tambua kwamba sipo kwa ajili ya kuwa maarufu na wala sikuhitaji watu kuweza kuujua uwezo wangu. Huyu aliye fanya hivi ni lazima nidili naye”

Magreth alizungumza kwa msisitizo huku akionekana kukasirishwa na video hiyo kusambaza kwenye mitandao ya kijamii. Akaingia chumbani kwake na kuiwasha simu yake ambayo toka asubuhi hakuwa ameisha kutokana na kuiweka kwenye chaji. Meseji mfululizo zikaanza kuingia kwenye simu yake huku zikiongozana na missed call kutoka kwa watu mbalimbali akiwemo raisi Mtenzi.

“Umeona sasa, watu kibado wame nitafuta”

Magreth alizungumza huku akirudi sebleni hapo.

“Nani na nani?”

“Hapa nina missed call mia moja na mbili, meseaji miatatu. Huko whatsapp ndio usiseme”

“Ina maana hii video ime samba sana”

“Ndio maana yake. Hembu fikiria watu ambao walimtuma huyo mtu wata kuwa kwenye hali gani sasa hivi, ni lazima atwakuwa wakinitafuta”

“Ila si alitumwa na Evans”

“Ndio kwani Evans yeye ana kikundi, si atakuwa amewalipa watu waifanye hiyo kazi je huyo mmiliki wa huyo mtu ata kuwa katika hali gani sasa hivi?”

Magreth alizungumza huku akikaa kwenye kiti kilichopo pembezoni mwa meza ya chakula.

“Mmmmm hapo ni kweli”

“Ndio maana nina kuambia kwamba hii video ni lazima ita kuwa ime niletea madhara makubwa ambayo kwa leo hayata onekana ila kwa baadae yata onekana. Heri ningekuwa nime zivaa zile nguo zangu basi ingekuwa ni jambo bora kuliko hapa ninavyo onekana sura yangu halisi”

Magreth aliendelea kulalama huku akiendelea kupitia meseji za watu walizo mtumia huku wengi wao wakionekana kumpongeza na wengine wakishangazwa kwamba ni yeye kweli au laa. Kengele ya getuni mwao ikaanza kuita na kuwafanya kutazamana. Magreth akaingia upande wa cctv kamera katika simu yake. Macho yakamtoka mara baada ya kuona shazi la waandishi wa habari wakiwa wamejazana getini kwake hapo.

“Ni nani?”

Josephine alimuuliza huku akimsogelea.

“Ona sasa waandishi wa habari na makamera yao wamefika hapa”

Josephine naye akatazama video hiyo inayo rekodiwa na kamera iliyopo getini hapo.

“Aisee sasa wame kuja kufanyaje?”

“Wame nifwata mimi ndio maana nikakuambia kwamba huyu aliye ituma hii video kwenye mtando ame kosea sana”

“Ngoja mimi nikazungumze nao”

“Uta wamabia nini?”

“Mungu ata niongoza kwa kile nitakacho waambia ila usitoke nje sawa”

“Poa”

Josephine akelekea getini, akufungua geti dogo na kuchungulia nje. Waandishi wa habari wakaanza kumpiga picha mfululizo huku wengine wakimuuliza maswali mfululizo.

“Jamani muna hitaji nini?”

Ikabidi Josephine kuwauliza wao swali moja kwa maana kila mmoja ana jitahidi kuzungumza anacho kijua yeye mwenyewe.

“Tuna muhitaji Magreth”

“Wa nini?”

“Kumuuliza juu ya hii video hapa”

“Mimi ni ndugu yake hivyo muna weza kuniuliza mimi nita wajibu”

“Je hii ni video ni yake au?”

“Siwezi kulijibu hilo swali”

“Je yeye ni askari au?”

“Sina maoni juu ya hilo.”

“Wengi wana sema kwamba hii ni filamu anayo iandaa?”

“Jamani nina ona kwamba hamuna maswali ya maana. Asubuhi njema”

Josephine mara baada ya kuzungumza hivyo akafunga geti hilo na kurudi ndani.

“Ume waambieaje?”

Simu ya Magreth ikaanza kuita, akaitazama kwa sekunde kadhaa na kuipokea huku akimtazama Josephine aliye shindwa kujibu swali alilo ulizwa, kutokana na kuingia kwa simu hiyo.

“Shikamoo muheshimiwa”

“Tupo salama”

“Kwa kweli siku muona muhisika wa hiyo video akirekodi”

“Sawa”

Magreth akakata simu yake.

“Nani?”

“Raisi”

“Anasemaje?”

“Alihisi labda nita kuwa nime husika katika kuirusha hiyo video kwenye mitandao”

“Mmmmm”

“Ndio hivyo nchi nzima kwa sasa ninaye tazamwa ni mimi na hilo lijambazi”

“Usijali mwanya kila jambo litakwenda sawa”

“Nataka msiba wa mke wa raisi ukiisha basi nidili na Evans popote pale alipo, basi nita shuhulika naye”

Magreth alizungumza kwa msisitizo huku akianza kunywa chai taratibu.

***

Mrs Sanga taratibu akamkabidhi simu yake mume wake huku ikiwa na video ya Magreth.

“Ni nini?”

Nabii Sanga alizungumza huku akiliweka pembeni gazeti alili kuwa ana lisoma.

“Tazama”

Nabii Sanga aka icheza(play) video hiyo na akaanza kumshuhudia Magreth jinsi anavyo pambana na Zuma. Uwezo wa Magreth katika kupigana kwa kweli ukampa kigugumizi nabii Sanga.

“Huyo ndio mtu ambaye una fikiria kudili naye”

“Hii video nani kakutumia?”

“Mwanao na ameniambia kwa sasa Magreth amesha ingizwa kwenye kitengo cha NSA na raisi ana mpenda kishenzi”

“Kwa hiyo ni agent wa serikali?”

“Hilo ndio jibu”

“Huyu mtoto amenitia hasara kubwa sana. Haki ya Mungu ni lazima nishuhulike naye ni lazima nimuue tu hata iweje?”

Mrs Sanga akamtazama mume wake jinsi anavyo nuwia kisha akaachia msunyo mkali unao onyesha kukerwa.

“Yaani unge jua jinsi unavyo nikera kwa kujibaragazua kwa maneno yako wala usinge zungumza”

“Kwa hiyo ulihitaji mimi nifanye?”

“Sijui”

Mrs Sanga alijibu kwa hasira na kutoka chumbani na kumuacha nabii Sanga akiwa amejawa na mshangao mkubwa sana. Mrs Sanga kabla hajashuka ngazi akarudi ndani kwake na kumpokonya mume wake simu hiyo.

“Nahitaji nafasi ya kupumzika so nakuomba usinisumbue kwa sasa”

Mrs Sanga alizungumza kwa jazba kisha akachukua pochi yake pamoja na funguo ya gari na kutoka ndani hapo. Hakuwasalimia hata baadhi ya watu walio fika katika kuhudhuria matanga ya misiba ya watoto wao. Akaingia kwenye gari lake na kuondoka nyumbani kwake huku moyo wake ukiwa umejawa na jazba kubwa sana kwani Magreth amekuwa ni kama mwiba ambao una mtonesha kila pale anapo muona.



Mrs Sanga akasimamisha gari lake pembezoni mwa barabara huku akiwa anamwagikwa na machozi. Vifo vya watoto wake wa kiume pamoja na ndugu zake hakika viana mfanya awe katuka wakati mgumu sana, wakati ambao hakuwahi kuupitia kwenye maisha yake. Siku zote alikuwa ana amani kwamba pesa na utajiri ni vitu vinavyo weza kumfanya binadamu kuwa na amani na furaha ila hadi ana shuhudia wanaye na ndugu zake wana ingizwa kwenye makaburi hakika akaweza kutambua kwamba pesa haziwezi kurudisha maisha ya walio potea. Simu yake ikaanza kuita, akaitazama kwa sekunde kadhaa kisha akakata kwa maana muda huo haitaji kabisa kuzungumza na mtu yoyote. Mrs Sanga taratibu akaondoka eneo hilo na kuanza safari ya kuelekea nje ya jiji la Dar es Salaam. Ndani ya lisaa moja na nusu akajikuta amefika katika mji wa Chalinze. Akatazama eneo hilo lenye barabara inayo elekea mkoa wa Morogoro huku nyingine inayo elekea katika mkoa wa Tanga.

Akakunja kushoto kwake na kuanza safari ya kueleeka mkoa wa Tanga kwa maana ana hitaji kuwa mbali na nyumbani kwake na ana hitaji kupata muda mzuri sana wa kupumzisha kichwa chake.

***

“Muheshimiwa raisi maandalizi yote ya mazishi ya makamu wa raisi yamekamilika.”

Sekretari wa raisi Mtenzi alizungumza huku akimkabidhi faili maalumu la matumizi yote yaliyo fanywa katika maandalizi hayo hayo pamoja na viongozi kutoka mataifa mengine ambao wata wasili nchini Tanzania siku tatu zijazo kwa ajili ya mazishi hayo.

“Makamu wa raisi wa Marekani naye ana kuja?”

“Ndio muheshimiwa hiyo taarifa tume pewa dakika ishirini zilizo pita”

“Ana kuja lini?”

“Kesho muheshimiwa”

“Hembu wapigie simu washauri wangu wote watano waweze kufika hapa tulijadili hili kwa maana hawawezi kutoa taarifa pasipo kunifahamisha mimi raisi”

“Sawa muheshimiwa”

Ndani ya muda mchache Josephine pamoja na washauri wengine wakaingia ofisini kwa raisi Mtenzi.

“Kuna jambo nina omba tuweze kudiliana hapa na nahitaji kupokea mawazo yenu”

“Jambo gani muheshimiwa?”

Mr the Brain aliuliza huku akimtazama raisi Mtenzi usoni mwake.

“Makamu wa raisi wa nchi ya Marekani naye ata kuwa ni miongoni mwa watu watakao hudhuria mazishi ya makamu wa raisi. Habari ime tolewa muda mchache na imetolewa kwa sekretari wangu pasipo kujulishwa moja kwa moja kwangu”

“Au wame mtuma makamu wao kuja kusuluhisha huu mgogoro unao endelea?”

Mzee Mbogo alizungumza.

“Nahisi”

Mr the Brain naye alijibu.

“Wamarekeni ni watu wajanja sana”

Josephine alizungumza na kuwafanya watu wote kumtazama akiwemo Julieth ambaye bado hana uelewa ukubwa wa jambo linalo endelea kati ya mataifa hayo mawili, Marekani na Tanzania.

“Kwa nini una zungumza hivyo?”

Raisi Mtenzi auliza.

“Ana kuja, moja kukuomba kwamba uweze kuwaachia wanajeshi wake walio tuvamia siku ile usiku. Pia ana kuja kuomba kuendelea kuwaruhusu wanajeshi wao kuendelea na ujenzi wa jiji hili la Dar es Salaam. Muamvuli wa mambo hayo yote ni huu msiba ambao dunia nzima ina tambua kwamba makamu wetu wa raisi ame fariki duniani”

Josephine alizungumza na kumfanya raisi Mtenzi kushusha pumzi taratibu kwa maana hadi sasa hivi bado eneo walipo wanajeshi hao Wamarekani, limezungukwa na vikosi vya jeshi la Tanzania na hakuna mwanayeshi anaye ruhusiwa kutoka nje ya kambi hiyo.

“Samahani jamani. Mimi nimgeni kwenye hili, jambo. Je ni kwanini tuna mfakano na nchi ya Marekani”

Julieth aliuliza kwa sauti ya upole.

“Ohoo pole sana, nilikuwa nime sahau kukufahamisha juu ya hilo. Wamarekani wameleta wanajeshi wao hapa nchini Tanzania kwa ajili ya kulijenga upya jiji la Dar es Salaam. Makubaliano ya kuja kwao yalifanywa na makamu wangu wa raisi ambaye kwa sasa ni marehemu. Ila nilipo kuja kugundua lengo na nia yao dhabiti ya wao kuja nchini kwetu nikapata mashaka na nikaamua kufnaya maamuzi ya kuwaondoa nchini kwangu. Ila raisi wao alionekana kukataa na kupinga maamuzi yangu na ikapelekea akapanga mpango wa kunia na pia walipandikiza kinasa sauti ndani ya ofisi yangu na kila kitu tulicho kuwa tuna kizungumza ndani ya ofisi hii walikuwa wana kisikia.. Tume washikilia wanajeshi ambao walitumwa kutua huku wale wangine walio kuja kwa lengo la ujenzi wakiwa chini ya ulinzi mkali wa vikosi vyetu vya ulinzi na hadi tunavyo zungumza hivi sasa. Kambi yao ime zungukwa na wanajeshi wetu”

Raisi Mtenzi alizungumza kwa kifupi ili kumpa Julieth ufafanuzi.

“Sasa kwa nini wana ng’ang’ania kujenga ikiwa nchi sio ya kwao?”

Julieth aliuliza tena.

“Lengo lao ni kuhitaji kuchukua hadhina ambayo ipo ndani ya nchi hii katika eneo la….”

“Ahaa muheshimiwa samahani ngoja nimfafanulie”

Josephine alizungumza huku akimtazama raisi Mtenzi usoni mwake. Raisi Mtenzi akamkubalia kwa kumpa ishara ya kuendelea kuzungumza.

“Kuna hadhina kubwa sana ndani ya nchi ya Tanzania ambayo endapo nchi ya Marekani wata ipata basi watakuwa ni matajiri mara dufu na watakuwa na nguvu pia. Ila sisi pia tukiipaa hiyo hadhina basi tuta pata nguvu na tuna weza kuwa nchi kubwa na yenye nguvu Afrika na duniani kwa ujumla.”

“Ahaa, hiyo hadhina ipo wapi?”

Julieth aliuliza huku akiwa amejawa na shahuku kubwa sana.

“Bado hatujajua”

Jibu la Josephine likamfanya raisi Mtenzi, mr Brain pamoja na mzee Mbogo kumtazama kwa mshangao kidogo.

“Ahaa sawa sawa. Hapo nime elewa mada inayo endelea”

Julieth alijibu huku akilini mwake akianza kutengeneza mazingira ya jinsi atakavyo ipata hiyo hadhina kwa manufaa yake yeye mwenyewe.

“Muheshimiwa raisi mimi nina ona tumuache makamu wake aje na kwa kile walicho kifanya basi tuta jua nini cha kuwabananisha kuhakikisha kwamba tuna endelea kuwakazia juu ya msimamno wetu tulio nao”

Mr Brain alishauri.

“Ni wazo zuri naliunga mkono”

Josephine naye alizungumza.

“Ila kuja kwake ina bidi kuhakikisha kwamba muheshimiwa raisi tuna kuwekea ulinzi mzuri na wakutosha kwa maana wana weza kufanya lolote wale jamaa”

Mzee Mbogo alizungumza huku akimtazama raisi Mtenzi.

“Mimi pia muheshimiwa nina ona tumuache makamu wao wa raisi aweze kuja”

“Sawa kama mume kubaliana kwenye hilo. Akaribie Tanzania, jambo la msingi tuhakikishe kwamba tuna shikamana kwenye kila aina ya maamuzi ambayo nita kwenda kutafanya”

“Usijali muheshimiwa tupo pamoja nawe”

“Sawa muna weza kuendelea na kazi”

Taratibu wakaanza kutoka ofisini hapo.

“Josephine nakuomba”

Raisi Mtenzi alimzuia Josephine na kumfanya arudi na kukaa kweye kiti alicho kuwa amekali. Walipo toka watu wote, raisi Mtenzi akamtazama Josephine usoni mwake.

“Kwa nini uliamua kumjibu vile Julieth ikiwa ni miongoni mwa washauri wangu na wasiri wangu”

“Muheshimiwa nina kuomba sana uweze kunisamehe. Ila ukweli ni kwamba simuamini kabisa Julieth”

Raisi Mtenzi akashusha pumzi huku akimtazama Josephine usoni mwake.

“Kwa nini humuamini?”

“Uta nishangaa sana kwa kukuambia kwamba sina sababu ya kunifanya nishindwe kumuamini sana. Ila tafadhali nina kuomba umpatie muda katika haya mambo na tusiwe tuna mueleza vitu vya ndani sana vinavyo endelea”

“Sawa nime kuelewa katika hilo. Je kuna jengine ambalo ume onyeshwa?”

“Hapana ila nikionyeshwa basi nita kuambia moja kwa moja”

“Sawa ila nina hitaji kukupatia kazi moja”

“Kazi gani muheshimiwa”

“Hakikisha macho yako yote mawili yana kuwa sambaba na Julieth, ili kama ni kujiridhisha katika kuto muamini basi wewe uwe wa kwanza, na kama uta ridhika katika kumuamini basi uwe wa pili katika hilo kwa maana mimi nina muamini na nina itambua familia yake ni watu wa dini na ambao hawana shida yoyote na mtu”

“Sawa muheshimiwa. Ila samahani katika hilo”

“Hapana usijali kwa maana hata tupo kwa ajili ya manufaa ya nchi na sio ya mtu mmoja au kuwatazama watu fulani. Alafu vipi ile familia ya wahusika wa haya mashambulizi ume weza kuonyeshwa?”

“Bado muheshimiwa ila nina imani muda wake utakapo fika basi wewe mwenyewe uta fahamu”

“Sawa kazi njema”

“Nashukuru”

“Alafu jambo jengine Jose. Mage ana endeleaje?”

“Bado ana umizwa na ile video iliyo samba”

“Nime toa jukumu kwa watu wangu wa I.T kuhakikisha kwamba wana mpata muhusika aliye rekodi na kupost ile video kwenye mtandao”

“Sawa muheshimiwa alafu kuna swala jengine”

“Swala gani?”

“Magreth amekabidhi jukumu la kumsaka Evans popote pale alipo duniani.”

“Hiyo ripoti nilikabidhiwa asubuhi na mzee Mbogo nami nime afiki juu ya hilo kwa maana ana uwezo na ana jua nini anacho kifanya”

“Sawa”

Josephine akatoka ofisini hapo na moja kwa moja akaelekea ofisini kwake. Julieth akazunguka mara kadhaa kwenye kiti chake huku akiwa amejawa na tabasamu pana usoni mwake.

‘Kabla hawajaipata hiyo hadhina ni lazima niipate’

Julieth alizungumza hukua akijaribu kutafakari nini cha kufanya. Akaitafuta namba ya baba yake na kumpigia kwa maana yeye ndio master plan wa mambo makubwa kama hayo.

“Baba shikamoo”

“Marahaba vipi?”

“Safi. Mbona una zungumza kinyonge una umwa?”

“Hapana, ila mama yako ameondoka nyumbani hapa kwa hasira. Sijui ni wapi anapo kwenda, na nikijaribu kumpigia simu zangu ana nikatia”

“Chanzo ni nini?”

“Video uliyo mtumia ana taka kuyapeleka mambo haraka haraka”

“Ohoo naelewa baba. Ila kuwa katika hali ya kawaida, mama ni mtu mzima na hato patwa na jambo lolote huko aendapo. Ila nina good news”

“Ipi tena?”

“Hatuwezi kuzungumza kwenye simu. Ila kama ina wezekana nina kuomba uweze kuja ikulu”

“Hapana mwanangu, kichwa changu nakiona hakipo sawa. Ila wewe ndio uje nyumbani kwa maana ni jana tu tume toka kuzika, hivyo aga kwa baba mkwe wako kwamba una kuja nyumbani”

“Sawa baba”

Julieth akakata simu kwa haraka. Akaelekea ofisini kwa baba yake mkwe.

“Ndio Julieth”

Raisi Mtenzi alizungumza huku akimtazama Julieth usoni mwake.

“Baba nina kuomba, niweze kwenda nyumbani. Baba yupo peke yake na mama ameondoka nyumbani kwa hasira hivyo kidogo naomba nikawaweke sawa”

“Oohoo kwa ile misiba iliyo tokea natambua ni hali gani ambayo mama ata kuwa ana pitia. Basi hakuna tatizo, wewe kakae na baba na mama uwaweka sawa. Ila mimi kiofisi nime kupa ruhusa, ila sina mamlaka na wewe. Labda ukamuombe ruhusa mume wako na akikukubalia basi hakikisheni kwamba muna ondoka na walinzi wa kutosha”

“Sawa baba nashukuru sana kwa hilo”

“Haya ila kumbuka kwamba kesho kutwa tuna msiba wa kumzika makamu wa raisi”

“Sawa baba”

Julieth akatoka ofisini hapo kwa haraka kwa bahati nzuri akakutana na Jery kwenye kordo wakakubaliana na wakondoka ikulu wakiwa na gari tatu huku gari mbili zikiwa na walinzi na gari waliyo ipanda ikiwa dereva pamoja na mlinzi mmoja aliye kaa siti ya mbele. Wakafika nyumbani kwa nabii Sanga na Julieth wakapokelewa na marafiki walio fika hapo nyumbani kuendelea kumfariji nabii Sanga.

“Baba”

Jlieth alizungumza huku akikumbatiana na baba yake.

“Vipi?”

“Safi”

“Shikamoo baba”

Jery naye alisalimia kwa heshima zote.

“Marahaba. Julieth naomba tuzungumze”

Nabii Sanga alizungumza na wakapandisha gorofani na kuingia chumbani kwa nabii Sanga.

“Ume jaribu kumpigia simu mama yako?”

“Hapana”

“Hembu mpigie na wewe?”

“Baba natambua mama ana hasira hivi sasa. Tumpatie muda akae huko, akitulia ata rudi. Ila nime kuja na jambo moja muhimu sana baba”

“Jambo gani?”

“Nchi ya Tanzania na Marekani zina mgogoro”

“Mgogoro wa nini!!?”

“Kuna hadhina ipo ndani ya nchi ya Tanzania. Wamarekani wana ihitaji na endapo wata ipata wana kuwa matajiri sana na endapo sisi pia Watanzania tuta ipata basi tuta kuwa matajiri sana. Ila nina hitaji nchi hizi zote mbili tuziwahi baba. Hiyo hadhina nina ihitaji tuijue ilipo na tuichukue na nina imani kwamba tuta kuwa na pesa nyingi kuliko hata huyo tajiri namba moja duniania”

Nabii Sanga akajawa na mshangao na baada ya sekunde kadhaa akaachia tabasamu pana sana usoni mwake kwa maana kile alicho kuwa amemuagiza mwanaye huyo wa kike kwenda kukifanya ndani ya ofisi ya raisi ndio hichi anacho kisikia tena kwa muda mchache sana ambao Julieth ame fanya kazi ndani ya ofisi ya raisi Mtenzi.

mtonesha kila pale anapo muona.



“That is my gilr, come here”(Huyo ndio msichana wangu, njoo hapa)

Nabii Sanga alizungumza kwa furaha na taratibu Julieth akaka pembeni yake na kumkumbatia.

“So baba mpango wetu hapa ni upi?”

“Mmmm ume sema kwamba Tanzania na Marekani zipo kwenye mgororo?”

“Ndio na makamu wao wa raisi ana kuja kesho kutwa kujaribu kukaa mezani na raisi Mtenzi kujua wana suluhisha vipi hili jambo”

Nabii Sanga akaa kimya huku akijaribu kupanga na kupangua mpango upi utaweza kutekelezwa ndani ya siku mbili hizo.

“Huu mgogoro ina bidi tuhakikishe tuna uongeza mara dufu”

“Una maana gani?”

“Ni lazima tuhakikishe kwamba makamu wa raisi wa Marekani ana fia hapa Tanzania”

Wazo hilo la nabii Sanga likamstua kidogo Julieth.

“Baba hilo kweli lita wezekana?”

“Ndio”

“Kivipi?”

“Ni lazima tuhakikishe kwamba tuna zipata zile nguo za Magreth au tutengeneze kama zile anazo zivaa na kujifanya spiderman wa Tanzania. Baada ya hapo tuna mvisha muuaji ambaye ata fanya jambo hilo na moja kwa moja hilo swala lita muangukia Magreth. Kiufupi tuta kuwa tume ua ndege wawili kwa jiwe moja. Magreth ata fungwa huku nchi zikiendelea kujawa na mitafaruku, na sisi itakuwa ni nafasi yetu kwanza kuingiza mizigo yetu kama kawaida na mbili kuhakikisha tuna ifahamu sehemu yenye hadhina hiyo na tuna chukua mambo kiulaini”

“Babab yaani wewe ni genius. Sikutegemea kama uta fikiria kama jambo hilo?”

“Ndio maana nime ongoza ogarnization yangu ya madawa ya kulevya na hapakuwa na hata kijana wangu aliye kamatwa. Wewe ume rithi akili zangu ndio maana nime kurithisha”

“Nashukuru baba, nini kupenda sana baba”

“Nina kupenda pia mwanangu”

Nabii Sanga na Julieth waakumbatiana huku wakiwa na furaha kubwa juu ya mpango huo walio ujadili.

“Ehee nani ambaye ata kuwa ni muuaji wa makamu wa raisi wa Marekani”

“Kuna sniper mmoja mwanamke na uzuri ana umbo kama la Magreth. Nita wasiliana naye ata ifanya kazi hiyo”

“Yupo wapi?”

“Yeye ni Mkenya. So ni kitendo cha kumpigia simu na kumuomba aweze kufika. Picha ya hizo nguo nita hakikisha nina mpatia fundi wetu azishone kwa uharaka sana nina imani ndani ya masaa kadhaa ata kuwa amezimaliza kuzishona”

“Sawa baba, mimi kazi yangu ni kuhakikisha nina kupatia full detail za ujio wake. Ata lala wapi, ata fikia wapi na ata kwenda wapi na muda gani?”

“Sawa ila kuwa makini sana na hakikisha kwamba lugha yetu tutakayo kuwa tuna zungumza kwenye simu isiwe ina ashiria kabisa kwamba kuna jambo lolote tuna zungumzia kuhusiana na ujio wa huyo makamu wa raisi wa Marekani”

“Sawa baba, ngoja nikaae na Jery”

“Ume kuja naye?”

“Ndio yupo sebleni na watu wengine”

“Vipi amegundua kwamba bikra yako ni bandia?”

“Hapana hadi sasa hatujafanya chochote”

“Kwa nini?”

“Nilimuambia kwamba tuta fanya mara baada ya kumaliza kumzika mama yake na amenielewa na kunikubalia katika hilo”

“Sawa, ila hakikisha kwamba haupati ujauzito kwa sasa hadi haya mambo yatakapo kwisha”

“Usijali baba, alafu nina hisi kwamba kama simpendi huyu mwanaume”

Kauli ya Julieth ikamfana nabii Sanga kumtaza kwa sekunde kadhaa Julieth kisha akaishika mikono yake miwili.

“Kwa nini?”

“Unajua kurudi kwake, kufunga kwetu ndoa kume kuwa kama mambo yaliyo kimbia spidi na kutokana na huu mpango ilinibidi kumkubalia”

“Niangalie”

Julieth taratibu akamtazama baba yake usoni mwake.

“Kama hayupo moyoni mwako. Hakikisha kwamba hili jambo linapo kwisha una MUUA ili kuhakikisha kwamba hakujui uhalisia wako. Umenielewa?”

Nabii Sanga alizungumza kwa sauti ya upole ila iliyo jaa ushawishi ndani yake.

“Nime kuelewa baba”

“Usifanye kosa katika hili mwanangu”

“Usijali baba una nijua vizuri. Je huu mpango tumshirikishe mama?”

“Hapana mama yako muache kwanza akili yake imkae sawa. Kufiwa na watoto wawili kwa mpigo ni jambo ambalo lina mtafuna kisaikolojia”

“Hata baba mkwe aliniambia hivyo na amenipa muda wa kukaa nyumbani kuhakikisha kwamba nina waweka sawa”

“Sawa sawa. Haya nenda kakae na mwenzako”

Julieth akambusu baba yake kwenye paji la uso kisha akatoka ndani hapo. Nabii Sanga akafungua shelf yake iliyo jengewa ukutani na akatoa note book yake ndogo. Akaitafuta namba ya muuaji huyo wa kike aishie nchini Kenya na akampigia.

“Niambie mpenzi”

Sauti nyororo ya kike ilisikika.

“Safi, sauti yako haijabadilika?”

“Sasa wataka niwe na sauti kama dume. Mimi ni manzi tena mrembo hivyo ni kawaida kuzungumza na sauti nzuri”

“Hahaaa, sasa una ratiba gani?”

“Nipo tu, ila pole bwana kwa vifo vya wana familia yako?”

“Nashukuru. Nakuhitaji uweze kuja Tanzania leo”

“Kimapenzi au kikazi?”

“Vyote vyote”

“Poa poa basi wacha niweke mafuta car yangu. Nikipiga fimbo hadi saa sita usiku nita kuwa Tz, si uta kuja hoteli au mke wako ata sumbua wewe?”

“Nita kuja”

“Basi najipanga”

“Poa poa”

“Badae”

Nabii Sanga akakata simu huku akiwa na furaha kubwa sana kwani mambo yake yana zidi kumnyookea na hiyo ndio nafasi ya kuhakikisha ana muondoka Magreth kwenye sura ya dunia.

***

Majira ya saa nane mchana mrs Sanga akafika jijini Tanga. Akasimamisha gari lake eneo la Kwaminchi huku akitazama hoteli iliyopo eneo hilo.

“Karibu sana hapa”

Mrs Sanga alizungumza huku akifunga mlango wa siti ya gari lake. Akafungua mkoba wake na kutoa miwani yake nyeusi, akaivaa na akashuka kwenye gari.

“Habari zenu vijana?”

Mrs Sanga aliwasalimia vijana walipo eneo hilo.

“Salama mama”

“Hapa Tanga kuna hoteli gani tofauti na hii?”

“Ahaa kuna hoteli nyingi sana mama. Labda una hitaji hoteli ya aina gani?”

Kijana mmoja mchangamfu alizungumza huku akimtazama mrs Sanga usoni mwake.

“Hoteli yenye hadhi ya juu kabisa”

“Kwa Tanga kuna hoteli ina itwa Tanga Beach resort na nyinge…..”

“Ipo pembezoni mwa bahari?”

“Ndio mama”

“Una weza kunipeleka”

Vijana hao wakamtazama mwenzao huyo anaye muelekeza mrs Sanga huku wakionekana kuwa na wasiwasi mwingi.

“No usiogope mimi ni mtu mwema”

“Ahaa labda nitumie usafiri wangu wa pikipiki ule pale”

“Ila sio mbali na hapa?”

“Ni mbali kidogo”

“Sawa nita kuwa nina kufwata kwa nyuma”

“Ila si uta nilipa?”

“Hilo halina shaka”

“Sawa mama”

Kijana huyo akaelekea kwenye pikipiki yake aina ya Watco. Akaiwasha na kuanza kuondoka huku mrs Sanga naye akimfwata kwa nyuma kwa mwendo wa taratibu.

‘Tanga ime badilika sana’

Mrs Sanga alizungumza kimoyo moyo kwa maana ni miaka mingi sana ime pita toka atembelee mkoa huo. Wakafika katika hoteli hiyo na taratibu mrs Sanga akasimamisha gari lake kwenye maegesho ya magari kwa muonekano wa nje wa hoteli hiyo, akaridhishwa kabisa kwamba sehemu hiyo ni sahihi kwa yeye kuweza kupata huduma ya kupumzisha kichwa chake. Akashuka kwenye gari lake, akafungua pochi yake na kutoa noti tano za elfu kumi kumi na kumkabi kijana huyo ambaye alijikuta akipatwa na kigugumizi kwa maana amelipwa kiasi kikubwa sana tofauti na kile alicho kuwa amepanga kumuambia.

“Una itwa nani kijana?”

“Tuma…..Tumaini”

“Nipatie namba yako kwa maana nita kuwa nina hitaji mwenyeji wa kunielekeza baadhi ya maeneo”

“Sawa mama una weza kuandika”

Mrs Sanga akatoa simu yake na kuanza kuinakili namba ya Tumaini. Akajaribu kuipiga na kijana huyo akatoa simu ndogo aina ya Nokia Obama ambayo ime zungushiwa raberband ili mfuniko wa nyuma usitoke.

“Namba yako ndio hii inayo ishiwa na hamsini na tatu?”

“Ndio. Nashukuru sana kijana”

“Asante nawe mama, niisave nani?”

“Save tu mgeni”

“Ndio jina lako?”

“Hapana yaani mgeni kwa maana ya mgeni aliye kuja Tanga”

“Ahaa….sawa sawa mama”

Tumaini mara baada ya kukamilisha kuinakili namba ya mrs Sanga. Akapanda pikipi yake na kuondoka huku moyoni akiwa ametawaliwa na furaha kubwa sana. Mrs Sanga akakodisha chumba chenye hadhi yake aliyo hisi kwamba ina mfaa na hakuhitaji usumbufu zaidi ya kupanda kitandani na kulala, kwa maana ame choka sana na uendeshaji wa gari kwa safari ndefu.

***


ITAENDELEA



0 comments:

Post a Comment

BLOG