Search This Blog

Wednesday, November 18, 2020

X SEHEMU YA 1/10

  


X  

WRITER…………………………………………EDDAZARIA G.MSULWA


WEBSITE………………………………………… www.storyzaeddytz.com
CONTACT……………………………………….. 0657072588/0768516188
AGE……………..18+

SEHEMU YA 1 KATI YA 10



“Haya sasa bwana harusi una weza kumbusu bibi harusi”

Mchungaji wa kanisa hili la KKKT alizungumza huku akitutazama mimi na mke wangu halali kwa sasa katika nyuso zetu. Taratibu nika mgeukia mke wangu huku sote tukiwa tumejawa na tabasamu kwenye nyuso zetu. Nikamshika mashavu yake malaini kisha nikaanza kumnyonya denda, lililo wafanya watu wote kanisani hapa kushangilia kwa furaha, huku matarumbeta yakijumuika nao katika shangwe hizo.

“Ina tosha sasa”

Mchungaji alizungumza kwa sauti ya chini na kutufanya mimi na mke wangu kuachiana kwa maana tume tumia zaidi ya dakika mbili kumyonyana denda hilo. Tukamaliza hatua ya mwisho ambayo ni kutia sahihi katika vyeti vyetu vya ndoa sisi na wasimamizi wetu kisha tukatoka kanisani hapa.

“Hongereni sana”

Baadhi ya marafiki zangu ambao ni madereva taksi wezangu walizungumza huku nao wakiwa na furaha kubwa sana. Karibia taksi mia mbili zikaanza msafara kutoka kanisani huku mimi, mke wangu pamoja na wasimamizi wangu wa harusi na dereva tukiwa katika taksi yangu ambayo nina imiliki. Hakika umoja wetu wa madereva taksi ume weza kunifanya nijisikie furaha sana kwa maana sina baba, mama wala ndugu wa tumbo moja. Watu ninao wafahamu ni madereva taksi wezangu, pamoja na baadhi ya wezangu tulio lelewa katika kituo cha watoto yatima Makete.

“Najisikia furaha sana kuwa na wewe mume wangu”

Mke wangu alizungumza huku akiwa amekilaza kichwa chake katika bega la mkono wangu wa kulia.

“Hata mimi nina shukuru mke wangu leo hii ume timiza ndoto yangu ya kwamba nami siku moja nita kuwa na mke ambaye ata nizalia watoto ambao wata ishi maisha mazuri”

“Amen Mungu atujalie mume wangu”

Tukafika katika hoteli moja ya kifahari kwa ajili ya kupiga picha kadhaa kabla ya kuelekea ukumbini. Karibia marafiki zangu wote ambao ni madereva taksi tukapiga nao picha.

“Kaka leo lazima tukuogeshe maji bwana, tuna kukaribisha kwenye ndoa, ume kimbia ubachela”

Mmoja wa marafiki zangu alizungumza huku akitutazama mimi na mke wangu.

“Hahaa jamani ndugu zangu maji si siku ya birthday?”

“Ohoo muulize Ngosha, yeye na mke wake tuli wamwagia maji siku ya harusi yao. Huo ndio utaratibu”

Marafiki zangu hawa walizungumza kwa furaha kiasi cha kunifanya nizidi kujawa na furaha. Baada ya mapumziko ya masaa mawili hotelini hapo, tuka anza safari sasa ya kuelekea ukumbini huku nikiwa na hamu sana ya kuona jinsi rafiki zangu hawa walivyo niandalia ukumbi wa harusi kwa maana wao ndio wana kamati wakubwa wa sherehe hii.

Kila muda macho yangu yana kazi ya kuutazama uzuri wa mke wangu ambaye asili yake ni muarabu wa Oman. Baba na mama yake wote ni watu wa Oman, ambao makazi yao kwa miaka zaidi ya ishirini na sita sasa ni hapa jijini Dar es Salaam huku, wakiwa wana milikia baadhi ya miradi mikubwa.

“Baby”

Mke wangu aliniita huku akinitazama usoni mwangu.

“Niambie mke wangu”

“Natamani sana kama baba na mama wange fika katika harusi yetu. Ila nasikitika kwa maana bado wana itikadi za kizamani kwamba sipaswi koelewa na mwanaume mweusi na isitoshe nime badilisha dini na kuwa mkristo”

Mke wangu alizungumza kwa masikitiko mengi sana kwa maana ndugu zake wame isusia harusi hii kwa sababu ya ubaguzi wa rangi na isitoshe hata kazi yangu ya udereva taksi hawajaipenda kabisa na kwa mara kadhaa wame kuwa wakiniita masikini.

“Usijali mke wangu. Maamuzi uliyo yafanya ni sahihi, walisema sinto kuoa ila leo nime kuoa. Nime kuahidhi huto lala njaa, wala kuishi maisha ya shida kama wao wanavyo niona. Nita pambana kuhakikisha kwamba una ishi katika maisha mazuri wewe na wanangu ambao tuta wapata”

“Nashukuru sana mume wangu. Hakika uwepo wako kwangu ni muhumu sana”

“Hata wewe ni mtu muhimu sana kwangu”

Tukafika ukumbini na kukuta wageni waalikwa wakiwa wamesha anza kuingia ukumbini.

“Eddy”

Msimamizi wangu aliniita.

“Niambie kaka”

“Kweli una ishi na watu vizuri. Una jua watu ni wengi sana?”

“Yaa ni wengi ndugu yangu. Kuna kadi kama mia tano hivi nilizitoa kwa wateja wangu na asilimia tisini na tisa wote wametoa michangu na waliniahidi kufika hapa”

“Safi sana ndugu yangu, una jua sherehe ni watu”

“Ni kweli kaka”

Tukaa ndani ya gari hizi hadi muda wa kuingia ukumbini ukawasili. Tukaanza kucheza mziki wa kuingilia ukumbini huku kila mwenye simu yake akijitahidi kurekodi au kupiga picha kwa tukio ninalo lifanya mimi na mke wangu. Sherehe ikaanza huku muendesha sherehe MC akijitahidi kuendana na ratiba kama jinsi ilivyo pangwa. Hakika mimi na mke wangu hatukutarajia kama harusi yetu ita pendeza kwa namna hii. Rafiki zangu hakika waliweza kujitoa kwa hali na mali kuhakikisha kwamba nina jawa na furaha. Tukapokea zawadi kedekede kutoka kwa wageni pamoja na kamati ya harusi. Nikamuomba muendesha harusi(MC) maiki ili niweze kuzungumza mambo mawili matatu kwa wageni waalikwa na akanikabidhi.

“Habari za muda huu”

Walikwa wote wakaitikia.

“Nina washukuru sana kwa muda na wakati wenu ambao mume weza kuutenga kwa ajili ya kuhuduria katika harusi yangu mimi na mke wangu kipenzi.”

“Hakika mume weza kunionyesha upendo ambao sikuwahi kuupata kwenye kipindi kikubwa sana cha maisha yangu. Wengi wenu nina hisi muta kuwa muna jiuliza ni kwa nini hamjawaona wazazi wangu au ndugu zangu wa tmbo moja?”

Nikakaa kimya kidogo kisha nikaendelea kuzungumza.

“Mimi nillelewa katika kutuo cha watoto yatima huko Makete nikiwa mtoto mchanga kabisa. Walezi wangu waliweza kunieleza kwamba niliokotwa katika mtaro huku nikiwa ndani ya mfuko wa rambo”

Nikakaa kimya tena huku machozi yakinilenga lenga usoni mwangu. Watu wengi wakaonekana kusikitishwa na historia yangu.

“Hivyo nime ishi pasipo kutambua wazazi wangu na nime kua na ndugu na jamaa ambao ndio nyinyi nyote mulio kusanyika hapa ndani. Mume nifundisha yaliyo bora sana kwenye maisha yangu na yale ambayo hayakuwa bora basi niliweza kuyaacha”

“Nina mshukuru mke wangu kwa kuja maishani mwangu. Pasipo kujali hali yoyote ame weza kunikubali na kuishi nami kwenye maisha yangu. Nina kupenda sana mke wangu kipenzi na Mungu aendelee kukupa uvumilivu wa kuwa nami katika maisha yangu. Marafiki zangu wote nina washukuru hakika muna zidi kunionyesha thamani ya kuwa na marafiki sahihi kwenye maisha. Asanteni na usiku mwema na Mungu awabariki”

Wageni wote wakaanza kupiga makofi kwa shukrani zangu hizo chache. Sherehe ilipo karibia kuisha, ukafika wakati wa marafiki zangu kunimwagia maji mimi na mke wangu na hatukuwa na namna zaidi ya kukubali kumwagiwa ndoo za maji kadhaa na marafiki zangu hawa, kisha tukaruhusiwa sasa kuelekea katika hoteli ya Ledger Bahari Beach kwa ajili ya kuanza mapumziko na mke wangu yatakayo dumu kwa siku saba.

Kitendo cha kufungua mlango wa chumba chetu na kuingia ndani, nikaanza kumnyonya denda mke wangu, huku akianza kunivua koti langu lililo lowana maji. Nimfungua zipi ya shela lake na nikamvua na akabaki na nguo zake za ndani. Nikamlaza kitandani huku tukiendelea kunyonyana denda lililo tawaliwa na hisia kali sana za kimapenzi. Mlango ukanza kugongwa, kitendo kilicho tufanya tusitishe kunyonyana denda. Nikatazama saa ya ukutani na kukuta ni saa nane kasoro usiku.

“Ni nani?”

Mke wangu aliniuliza kwa sauti ya chini kidogo.

“Labda wata kuwa ni wezetu ngoja nika wasikilize.”

Nilizungumza huku nikishuka kitandani, nika funga vifungo vya sheti langu na kuufungua mlango taratibu na umakini mkubwa.

“Fuc**”

Nilijikuta nikiufunga mlango mara baada ya kuiona sura ya mlinzi wa makamu wa raisi.

“Ni nini mume wangu?”

Mke wangu alizungumza huku akikaa kitako kitandani.

“Usijali mke wangu, jifunike shuka”

Taratibu mke wangu alijifunika shuka huku akinitazama nikifungua mlango kwa mara nyingine na kutoka nnje na kuufunga mlango.

“Haloo Eddy, habari za siku nyingi”

“Salama ni nini kime kuleta hapa?”

“Mkuu yupo kwenye gari ana kuhitaji”

Nikashusha pumzi nyingi sana huku nikimtazama mlinzi huyu ambaye mimi na yeye tuna fahamiana vizuri sana.

“Nisubirie”

Nikarudi ndani na kumkuta mke wangu akiwa bado ana wasiwasi.

“Baby nina kuja sasa hivi. Funga mlango kwa ndani hadi pale nitakapo rudi. Nita gonga mlango mara mbili tu uta fungua, kama ita kuwa ni zaidi ya hapo usifungue”

“Una kwenda wapi mume wangu?”

Mke wangu aliuliza huku uso wake ukiwa na wasiwasi mkubwa sana.

“Kuna mtu nina zungumza naye. Samahani sana mke wangu sawa mama”

Nilizungumza kwa sauti ya mahaba huku nikimtazama mke wangu usoni mwake.

“Sawa”

Mke wangu alinijibu kwa unyonge.

“Kuwa makini Eddy now ni usiku”

“Usijali mama watoto”

Nilizungumza huku nikimnyonya denda kwa dakika moja nzima kisha nikashuka kitandani huku naye akinifwata kwa nyuma. Nikatoka na akafunga mlango kwa ndani, nikamtazama mlinzi huyu wa makamu wa raisi kwa dakika kadhaa kisha tukaanza kuongozana kulekea alipo makamu wa raisi. Tukafika kwenye maegesho ya magari ya hoteli hii na nika ingia kwenye gari aina ya Range Rover na kukaa siti ya nyuma, nika mkuta makamu wa raisi akiwa amekaa huku amevalia kofia ambayo sio raisi kwa mtu kumfahamu na isitoshe gari hii aliyo itumia ni binafsi na ame kuja na mlinzi wake mmoja tu.

“Shikamoo mkuu”

“Marahaba X. Hongera sana kwa harusi yako”

“Nina shukuru”

“Nina imani nime kuja wakati mbaya ila sikuwa na jinsi zaidi ya kuweza kufika muda huu”

“Usijali mkuu”

“Mke wako ana jua upande wako wa pili wa maisha?”

“Hapana”

“Safi na hapaswi kufahamu. Nime kuja na habari mbaya kwa taifa”

Nikajiandaa kisaikolojia kabisa kuipokea habari hiyo mbaya kwa maana hadi ukiona makamu wa raisi ameamua kunitafuta basi mambo ndani ya nchi basi sio mazuri.

“Majira ya saa nne usiku ndege ya raisi akitokea katika kikao cha kusuluhisha migogoro ya Sudan ya kusini kwa maana raisi wetu ndio mwenye kiti wa kutatua migogoro hiyo, ime weza kupotea katika mazingira ya kutatanisha kuanzia muda huo hatujaweza kufahamu ni wapi ndege yake ilipo hadi baada ya lisaa lililo pita ndipo tukagundua kwamba ndege ya rasi ime weza kutekwa”

Habari hiyo ika nistua sana kwa maana hadi kuona ndege ya raisi ina tekwa basi kuna mlolongo mrefu sana wa mpango huo. Nikashusha pumzi taratibu huku nikitazama jinsi makamu wa raisi akifungua brufcase na kutoa faili moja la rangi ya kaki pamoja na ipade kubwa kiasi.

“Samahani muheshimiwa makamu wa raisi. Ila mimi nilisha acha kazi na ni mwaka watatu sasa, nime ishia maisha ya kawaida na nina hitaji kuwa na familia yangu. Maisha ya mikiki mikiki tena nikiwa ndani ya ndoa kwa namna moja ama nyingine yana weza kuidhohofisha ndoa yangu ambayo kwa sasa ni changa na mbaya zaidi mke wangu hatambui maisha yangu ya nyuma hususani maisha yangu ya ujasusi”

Nilizungumza kwa msisitizo huku nikimtazama makamu wa raisi usoni mwake.

“Nina litambua hilo X, na hii nina kuomba iwe ni kazi yako ya mwisho kabisa, taifa lina hitaji msaada wako na hapa ninavyo zungumza raisi yupo kwenye wakati mgumu sana”

Makamu wa raisi alizungumza kwa suati ya upole sana huku akinitazama. Nikakaa kimya kwa dakika tatu huku nikifikiria jinsi wezangu watatu walivyo weza kuuwawa nchini Pakistani tukiwa katika moja ya oparesheni ya kijeshi inayo husiana na umoja wa mataifa. Katika shambulizi hilo la gafla ambalo nilipoteza rafiki zangu vipenzi sana na nilio wapenda na kushirikiana nao kwenye kazi nyingi sana, lilinifanya nikate tamaa kabisa ya kuendelea kutumikia nchi yangu pamoja na jeshi la umoja wa mataifa katika maswala ya kijasusi. Na nilipo rudi nchini Tanzania nikaamua kuishi maisha ya kaaida kabisa ya kuwa dereva taksi ambaye nilitokea kupendwa sana na madereva wezangu pamoja na wateja wangu ambao fadhila zao wame weza kunilipa katika harusi yangu ya leo.

“X”

Makamu wa raisi aliniita na kunifanya niweze kuzinduka kutoka katika dimbwi hilo la mawazo.

“Ndio mkuu”

“Sikuamrishi ila nina kuomba sana kwenye hili kwa maana hadi sasa hivi viongozi wa ngazi za juu tume tokea kupanic na hatujui ni nini cha kufanya. Wewe ndio mtu wa pekee utakaye tusaidia kumpata raisi”

Makamu wa raisi alizungumza kwa sauti ya chini sana na iliyo jaa unyonge.

“Nime kuelewa mkuu. Je mke wangu nina muagaje, ikiwa leo ni siku yetu ya harusi na tuna wiki moja ya kuishi kupumzika pasipo kufanya kazi yoyote?”

Makamu wa raisi akaka kimya kwa sekunde kadhaa kisha akanitazama usoni mwangu.

“Nina kuomba sana umueleze ukweli juu ya jambo hili?”

“Samahani mkuu ila sheria namba moja ya ujasusi ni kwamba hupaswi kujulikana wala kumueleza mtu yoyote hata kama ni mke wako wa ndoa. Pili ata jiuliza kwa nini nili mdanganya siku zote na nime amua kumueleza siku kama hii. Mke wangua ameweza kuchana na kila kitu kizuri kwao na ameamua kuungana nami kwenye haya maisha ya kawaida ambayo nina ishia naye. Sihitaji kumuumiza kwa maana nina mpenda na nina muhitaji na sinto hitaji kumuumiza. Hivyo samahani sana muheshimiwa, sinto weza kuichukua kazi hiyo kwa maana kuna kitengo kama TNS(Tanzania National Security) na vitengo vingine vingi sana mkuu. Wapeni kazi hiyo waweze kuifanya. Nilisha zika madhambi yangu yote, nilimwaga damu za watu wengi sana, nilifanya mambo machafu mengi sana hivyo sasa acha niishi kwenye maisha yampendezayo Mungu na mke wangu”

Mara baada ya kuzungumza hivyo nikashika kitasa cha mlango, kabla ya kufungua mlango makamu wa raisi akanishika mkono wangu wa kulia kwa maana amekaa upande wa kulia kwangu.

“Eddy”

Makamu wa raisi akaniita kwa jina langu la kawaida ambalo sio mara nyingi kulitumia kwani hupenda sana kuniita jina la X kwa maana kipindi nipo kazini ndio code tulizo kuwa tuna zitumia kuitana majina kwani kuna X, X1 hadi X3 ambao wezangu hao watatu wote wamesha tangulia mbele za haki katika shambulizi hilo la nchini Pakistani na mimi ndio X ambaye nime baki na nilikuwa ndio kiongozi wao.

“Naam”

“Nina zungumza kama mzazi. Nina kuomba unisikilize sana mwanangu, tuliweza kukuchukua kutoka katika kituo cha Makete ukiwa bado kijana mdogo sana. Wewe na wezako muliweza kupewa mafunzo ya hali ya juu ambayo hakuna mwana usalama yoyote hapa nchini Tanzania aliweza kupewa. Natambua una umia kwa ajili ya vifo vya wezako, ila nina kuomba ukumbuke kiapo ulicho kula cha kulilinda Taifa hadi kufa kwako, tafadhali Eddy fikiria hivyo”

Makamu wa raisi aliendelea kuzungumza kwa upole sana. Nikainamisha kichwa changu chini kwa sekunde kadhaa kisha nika mtazama usoni mwake.

“Tafadhali sana Eddy. Nchi kwa sasa ina kuhitaji wewe kwenye hili jambo, na hawa ndio watekaji walio mteka raisi, mke wake pamoja na wafanyakazi wengine walio kuwa ndani ya ndege ya raisi. Walinzi wake waliuwawa wote na hiyo ndio video iliyo weza kutumwa ikulu na kila baada ya lisaa moja wana muua mateka mmoja wana shinikiza nchi ya Tanzania iweze kujiondoa katika ushirika wa kutatua migogoro ya Sudan kusini. Na wamehitaji kiasi cha dola bilioni mbili nukta tano ndani ya msaa ishirini na nne na endapo tukishindwa kufanya hivyo basi watawaua mateka wote akiwemo raisi pamoja na mke wake”

Makamu wa raisi alizungumza huku akionionyesha mmoja wa wafanyakazi wa raisi wa kike ambaye kwa miaka ya nyuma alisha wahi kuwa demu wangu, akipigwa risasi ya kichwa na mmoja wa watekaji na akafa hapo hapo, kitendo kilicho nifanya nijikute kikikunja ngumi ya mkono wangu wa kushoto huku nikitetemeka kwa hasira kali sana kwa maana binti huyo ame uwawa kifo cha kinyama sana pasipo sababu ya msingi.



“Hii ndio hali halisi inayo endelea”

Makamu wa raisi alizungumza kwa sauti ya upole huku sote tukitazama video hiyo jinsi mateka wanavyo pigwa.

“Je mume weza kugundua ni kundi gani la kigaidi ambalo lina husika?”

“Hadi sasa hivi hatujajua ni kundi gani linalo husika katika jambo hili”

Nikaichukua ipade hiyo na kuanza kuitazama video ya mauaji ya wafanyakazi wa raisi.

“Hawa jamaa ni SPLM”

Nilizungumza huku nikiendelea kuwatazama wanajeshi hao.

“Ume juaje X?”

Makamu wa raisi aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.

“Hawa SPLM wana pambana sana na serikali yao. Sasa ukitazama hata lafudhi ya kuzungumza moja kwa moja una jua hii lafudhi ni ya Kisudan, japo wana jaribu kuzungumza kama wa Nigeria, ila ni watu wa South Sudan”

Nilizungumza kwa kujiamini kwa maana nina yafahamu makundi mengi sana ya kigaidi ndani ya nje ya bara la Afrika kwa maana kwa kipindi cha karibia miaka sita nilikuwa nina fanya kazi na umoja wa mataifa mimi na wapelelezi wezangu katika kupambana na makundi ya magaidi sugu ambayo wanajeshi wa kawaida huwa wana shindwa kuyakabili.

“Sasa ni kwa nini hawa SPLM wame mteka raisi wetu ikiwa ana jitahidi kuwakalisha chini wao na serikali yao kwa ajili ya kuwapatanisha?”

“Mkuu ukizungumza hivyo uta kuwa una shindwa kuelewa haya mambo yanayo kwenda. Ukitaka kulijua hilo, wewe jiulize ni kwa nini makundi ya Islamic State, Boko Haram, Al-Shabab na wengine wana kuwa wana pambana na serikali zao. Kitu kikubwa wanacho kitaka wao ni madaraka na si kingine. Hivyo jambo la msingi ni kwamba raisi wetu akisha okolewa katika hili akae pembeni kwa maana watu anao wasaidia ndio hao wana mrudia na kumteka”

“Nime kuelewa X. Nina kuomba sana uweze kumsaidia raisi?”

“Je ndege yake bado ipo angani au imesha shushwa ardhini?”

“Hatujajua kwa maana kama hapo unavyo ona hiyo video inaonyesha kwamba wapo ndani ya ndege?”

“Hii ndege haipo hewani”

Nilizungumza huku nikiitazama kwa umakini video hii.

“Sawa X watu wangu wa IT bado wana endelea kuitafuta kwa satelaite?”

“Hamuwezi kuipata kwa kuitafuta kwa Satelaite, kwa maana watekaji nao sio wajinga. Wamedhamiria kufanya hivyo. Je mume wasiliana na serikali ya South Sudan?”

“Bado hatujawasiliana nao kwa maana wao wenyewe hawana nguvu katika hili”

Nikashusha pumzi huku nikitafakari kwa sekunde kadhaa. Hakika tukio kama hili wakiende watu ambao hawana ujuzi mkubwa wana weza kufa.

“X tafadhali nina kuomba sana ukubali kuifanya kazi hii”

“Nime kuelewa. Ila nina condition”

“Zipi?”

“Moja nina hitaji mke wangu akakae ikulu hadi siku ambayo nita rudi kutoka katika kazi hii. Mbili endapo nita kufa mke wangu nina hitaji aweze kulipwa stahiki ninazo stahili kwa ajili ya kazi hii. Tatu nikiimaliza kazi hii sinto hitaji kuonana na wewe tena kwenye swala la kazi kama tukionana tuwe kwenye maisha ya kawaida.”

“Nime kubaliana na hayo yote”

“Sawa nina hitaji kuzungumza na mke wangu sasa hivi”

“Hakuna shaka nita kutumia gari liletwe hapa kwa ajili ya kuja kuwachukua”

“Sihitaji dereva, yeye aache funguo chini ya kapeti la gari upande wa dereva na saa moja kamili nita kuwa Ikulu”

“Nashukuru sana X”

“Asante nawe mkuu”

“Je nikuachie hii ipade?”

Nikaitazama kwa muda kidogo kisha nika shuka ndani ya gari huku nikiwa nime ishika ipade hii. Nikafika katika mlango wa chumba changu na nika gonga mara mbili kama nilivyo muahidi mke wangu, hazikuisha hata sekunde ishirini mke wangua akafungua mlango na nikaingia ndani. Mke wangu akanikumbatia kwa nguvu huku nikiyasikia jinsi mapigo yake ya moyo yanavyo dunda kwa nguvu sana.

“Mume wangu nilikuwa naogopa kukaa mwenyewe”

“Usijali mke wangu nime rudi, nilizungumza huku nikimuachia mke wangu na tukakaa kitandani.”

“Ipade ya nani hiyo?”

“Huwezi amini mke wangu nime toka kuonana na makamu wa raisi?”

“Weee!!?”

Mke wangu alishangaa mshangao ambao una ashiria kwamba haamini ninacho mueleza.

“Kweli vile mke wangu na ameondoka muda huu. Ameniambia kwamba kesho asubuhi tuweze kuelekea ikulu”

“Ngoja kwanza mume wangu. Makamu wa raisi wewe amekujuaje ikiwa wewe ni mtu wa kawaida sana?”

“Hahaaa una jua kazi yangu hii bwana, kuna siku nilimpakiza kwenye taksi yangu pasipo mimi kujua kwa maana alikuwa ame valia kizee sana na kuweka ndevu bandia. Sasa hapa ndio alikuwa ana niadhithia kwa maana nakumbuka nilimpeleka kwenye hospitali kama nne. Alinikodisha siku nzima kumbe alikuwa ana fanya ziara za kimya kimya mahospitalini”

“Duuu mume wangu ina bidi uwe makini sana kwa maana uta kuja kubeba hadi majambazi.”

“Ni kweli, jambo la msingi uniombee kwa Mungu aniepushe na mabalaa. Vipi ume kubali kwenda ikulu?”

Nilimuuliza mke wangu huku nikimtazama machoni mwake.

“Yaani nikikataa nita kua na mapungufu ya kiakili mume wangu. Hakuna Mtanzania yoyote wa kawaida, ukamueleza kwamba kuna safari ya ikulu alafu akakukatalia kwenda”

Mke wangu alizungumza kwa furaha iliyo nirahisishia mambo kwa maana yote niliyo mueleza kuhusiana na kukodishwa na waziri mkuu ni uongo. Ila kutokana mke wangu ana niamini sana hivyo ime kuwa ni rahisi sana kumshawishi. Mke wangu taratibu akanivua shati langu na tukaanza kunyonyana denda huku tukiwa katika hisia kali sana za kimapenzi. Taratibu nikaanza kumnyona kila kona ya mwili wake jambo ambalo siku zote mke wangu amekuwa akilipenda nimfanyie kabla ya kuingia katika uwanja wa mapenzi. Nilipo jiridhisha nimesha muandaa vya kutosha, tukaanza mtanange wa kukata na shoka, kitu ninacho kipenda kutoka kwa mwanamke huyu wa kiarabu ni kwamba ana nimuda makeke yangu ya kitandani. Hata nimpelekee mashamabulizi ya aina gani ana yahimili na kurudisha mashambulizi sawa na yale niliyo mpekea. Vilio vya kimahaba vya mke wangu siku zote huwa ndio vina nipagawisha kwa maana ana ushawishi una kufanya uzidi kumpa mambo matamu.

Hadi tuna maliza mzunguko wa kwanza ulio dumu kwa dakika arobaini na kitu, kila mtu akajilaza chali huku tukisikilizia jinsi upepo wa AC, unavyo tupuliza taratibu.

“Baby”

Mke wangu aliniita huku akijigeuza taratibu na kujilaza kifuani mwangu.

“Niambie mke wangu”

“Nakupenda sana, nita zidi kukupenda hadi kufa kwangu”

“Kweli?”

“Haki ya Mungu vile mume wangu. Ila nina kuomba usiniumize moyo wangu mume wangu”

“Siwezi kufanya hivyo mke wangu.”

“Baby”

“Naam”

“Niambie siri ambayo hujawahi kuniambia. Leo tuna anza maisha mapya ya ndoa yetu. Sihitaji kusikia siri hiyo kutoka kwa mtu yoyote zaidi ya kinywa chako. Sinto kulaumu wala kukasirika kwa maana nime weza kuisikia kutoka kwako. Najua leo sio mara ya kwanza kukuuliza hili swali mume wangu, ila kama hakuna ulicho nificha basi nafuraha kusika ukweli kuhusiana na wewe kwa maana mimi una tambua kila kitu cha maisha yangu ya nyuma”

Hakika swali hili la mke wangu ni mara ya tatu ana niuliza, alisha niuliza mara mbili tukiwa katika uchumba na leo ana niuliaza mara ya tatu tukiwa katika siku yetu ya kwanza katika maisha ya ndoa. Jambo baya ni kwamba makamu wa raisi ame niomba niweze kurudi kazini kwa ajili ya kumukoa raisi na kipindi cha nyuma niliweza kumficha mke wangu maisha yangu ya nyuma kwa sasabu nilikuwa sina mpango wa kurudi kazini tena.

Taratibu nikaa kitandani huku nikiwa nina jaribu kutafakari jinsi ya kuanza kumueleza mke wangu, maisha ambayo hakika nikimueleza ata niogopa na nina wasiwasi wa yeye kupunguza upendo wake kwangu.

“Baby”

Mke wangu aliniita huku akinitazama usoni.

“Yes honey”

“Kuna jambo una taka kuniambia?”

Nikatabasamu kidogo ili kumtoa wasiwasi kwa maana tayari amesha anza kunitazama kwa macho yake ya udadisi.

“Kuwa huru mume wangu, mimi nimesha kuwa mke wako, mimi ndio msiri wako na mimi ndio tulizo la moyo wako. Niambie tu sinto kasirika kabisa mume wangu”

“Mke wangu””

“Bee”

“Kwenye kila maisha ya bina damu kuna historia ya nyuma. Wapo wenye historia mbaya na wapo ambao wana historia nzuri”

“Ni kweli mume wangu”

“Nilikuadithia maisha yangu ya utotoni hadi nilipo fikisha umri miaka kumi na tano?”

“Ndio mume wangu”

“Kuto kuwa na wazazi kulinifanya nijikute nina ingia kwenye maisha ambayo sikuwahi kuyafikria kabisa”

“Maisha gani mume wangu?”

Mke wangu alizungumza huku akijilaza vizuri kifuani mwangu.

Nikakaa kimya kwa dakika mbili huku nikijiwaza ni anze wapi kumueleza mke wangu.

“Kuna siku mimi na rafiki zangu watatu ambao tulilelewa katika kitoo cha watoto yatima na tulikuwa na umri sawa, tulipanga kutoroka pale kituoni. Tulikuwa tuna sikia tu jiji la Dar es Salaam na tulitamani sana kuweza kufika Dar”

“Mimi ndio nilikuwa master mind. Niliweza kuandaa mfumo mzima wa kutoroka na kweli tulifanikiwa kumlipa mmoja wa madereva wa lori la mizigo na tukatoroka katika mkesha wa ChrisMars”

Mke wangu akatabasamu huku akinitazama usoni.

“Basi lile lori likukuwa ni la mbao. Katikati ya moja ya tera lake tuliwekewa kama kijikibanda ambacho kilitutosha kukaa watu wanne. Kipindi hicho tuna viji miili vidogo vidogo. Nakumbuka hiyo siku tuliiba ile mikate inaitwa Bofulo, pamoja na chupa za maji, hivyo ilikuwa ina tutosha kula katika safari yetu na kile kijibanda kilizungushiwa mbao hivyo haikuwa rahisi kwa askari kuweza kugundua jambo hili”

“Mmmm mume wangu mulikuwa na hatari”

“Yaa tulikuwa tumesha amua kwenda kuyaanza maisha mapya Dar es Saala na hakuna aliye kuwa na wazo la kurudi katika kituo”

“Ngoja kwanza mume wangu ni kwa nini muliamua kutoroka katika kituo kile ikiwa mulilelewa pale?”

“Tulikuwa hatupendi kusoma, pia maisha ya kuishi wengi, yaani muna chungwa kama vile gerezani. HIvyo hatukuyapenda maisha hayo”

“Ehee endelea mume wangu, kwa maana stori tamu”

“Hahaa. Basi tulifanikiwa kufika Dar es Salaam usiku wa tarehe ishirini na tano. Ishu ni kwamba hatukuwa tuna jua hata mtaa mmoja. Hata dereva aliye tupakiza alitueleza kwamba mkataba wetu na yeye ume ishia kwenye kutuleta tu Dar es Salaam hivyo yaliyo baki kila mmoja aweze kushika njia yake”

“Kama nina waona hapo”

“Yaani ila ilitubidi kuwa majasiri hususani mimi nilibidi kuwaongoza wezangu katika kupambana na mji huu. Tulijichanganya na watoto wa mitaani ambao walianza kutufundisha tabia za kukaba, kuiba, kupora na kadhalika”

“Masikini weee”

“Ndio hivyo nilisha wahi kuwa kibaka mzoefu mumeo.”

“Natamani ninge kutana na wewe kipindi hicho nina imani ninge kusaidia kukutoa kwenye dimbwi hilo”

“Hata sasa hivi Mungu ametukutanisha kwa makusudia zaidi. Ina wezekana tunge kutana kipindi hicho ninge kukaba na wewe, nina imani unge kuwa wa kwanza kupiga kelele za mwizi”

“Hahaa ni kweli”

“Basi kuna siku moja mimi na wezangu hao watatu, tukapanga kwenda kuiba kwenye nyumba moja hivi ya kifahari. Sasa kumbe ile nyumba bwana ni ya mkuu wa jeshi na sisi wala hatukulijua hilo”

“Hahaaa ehee ikawaje mume wangu?”

Mke wangu alizungumza huku akijiweka vizuri kitandani na kunitazama kwa furaha kubwa sana.

“Kweli tulifanikiwa kuingia mule ndani kama majira ya saa sita hivi usiku. Una jua kipindi hicho tuna miaka kumi na saba hivi. Kumbe mzee aliweza kutuona bwana na ile nyumba yake alifunga kamera za ulizi za siri ambaso sio rahisi kuziona. Pia kulikuwa na taa kubwa zenye mwanga mkali sana, siku hiyo huyo mzee alikuwa hajaziwasha.”

“Sasa mume wangu mulipanga kwenda kuiba nini?”

“Chochote kitakacho tukalia vizuri sisi tulikuwa tuna bebe. Iwe ni tv enzi hizo yapo yale ma tv chogo, deki za vhs, redio yaani sisi ilikuwa somba somba. Mzee akatusubiria hadi tume maliza kuiba tumesha beba mizigo yetu. Sasa kutoka katika nyumba hadi ukuta kuna kajiuwanja karefu kidogo kwa maana mzee alikua na bonge moja la jumba”

“Yaani mume wangu, ehee ikawaje?”

“Tume fika katikati ya kiwanja bwana hayo mataa yakawashwa, una ona zile taa za uwanja wa taifa, mpira ukichezwa usiku, una ona kama mchana?”

“Yaa”

“Sasa ndio mambo yaliyo kuwa, tuliogopa wee acha tu. Mbaya zaidi mzee akapiga risasi hewani yaani hata nguvu za kukimbia zilitiishia”

“Hahaaaa”

“Kuna mwezetu mmoja alijikojolea live”

“Hahahaaa”

Mke wangu alizidi kucheka kwa furaha sana.

“Yaani asikuambie mtu, hiyo siku ndio niliamini, ingia kwenye kumi na nane za watu wote ila usiingie kwenye kumi na nane za wanajeshi. Tulikula mikanda ile ya jeshi, mzee aliturukisha kachura kachura huku kila mmoja akiwa amebeba mzigo wake alio iba. Mbaya mimi nilikuwa nina tv ya inch ishirini na mbili, mpanasoni chogo huo ni mzito balaa”

Mke wangu akazidi kucheka hadi machozi yakaanza kumwagika usoni mwake.

“Yaani ukiangusha tu, una kula mikanda, mabuti alfu ilikuwa ni kipigo cha mtu mmoja sipati picha kama wangekuwa wawili au watatu. Tulilia sana mke wangu, yaani asikuambie mtu, yaani kumbukumbu ya siku hiyo sitaki kuikumbuka kabisa kwenye kichwa changu”

“Hahaa masikini wee, pole mume wangu”

“Yaani lile varangati lilianza saa saba hadi saa kumi na mbili asubuhi. Yaani tulikuwa hoi, hata kunyanyuka tulishindwa.”

“Mzee huyo una mkumbuka?”

“Weee naachaje kumkumbuka kwa mfano”

“Yupo hai hadi leo?”

“Ndio yupo hai na ndio makamu wa raisi niliye toka kuonana naye”

“Weeee!!”

“Haki ya Mungu mke wangu, kipindi hicho makamu wa raisi alikuwa mkuu wa jeshi yaani asikuambie mtu nilijuta kwa nini nilitoroka Makete”

“Ehee akawafanyaje?”

“Pale kwake ana kama kaji stoo, alitufungia humo tukiwa chakari hatujielewi. Ninacho kumbuka alitufunga mule kama wiki moja na kwa siku tulikuwa tuna pata msosi mara moja tu.”

“Masikini”

“Yaani tulijiapiza kwamba tukitoka pale hatoto kuwa tena vibaka”

“Ehee ikawaje?”

Nikakaa kimya kwa sekunde kadhaa huku nikifikiria hatua hii ya ukweli ambayo nina kwenda kumueleza mke wangu, ata jisikiaje.

“Kuanzia kipindi hicho ndipo nilipo ingia kwenye maisha ambayo sikutegemea kama nita kuja kuyaishi”

“Maisha gani hayo?”

“Mzee aliweza kutuhoji mmoja baada ya mwengine na kila mtu kwa wakati wake. Alipo maliza kutohoji akatupeleka katika moja ya kambi ya jeshi ambayo sio maarufu na wala haijulikani kabisa kwa maana tulikwenda tukiwa tume fungwa vitambaa vyeusi”

“Mungu wangu aliwateka?”

“Yaani ni zaidi ya kutekwa”

“Masikini weee, hadi nina waonea huruma mume wangu”

“Yalisha pita na hichi inacho kwenda kukueleza mke wangu, tafadhali naomba usije ukafungua kinywa chako uka mueleza binadamu wa aina yoyote kwa maana wewe ndio mtu wa kwanza ninaye kueleza jambo hili ambalo ni siri kubwa sana kwenye maisha yangu na usalama wa nchi yangu”

Mke wangu macho yakamtoka huku akiwa amejawa na mshangao mkubwa sana kwa maana kipindi cha nyuma nilisha mueleza kipengele cha kuishi katika kituo cha watoto yatima na nika mueleza jinsi nilivyo anza maisha ya udereva taksi jijini Dar es Salaama ila kipengele cha kutoroka katika kitio hicho na maisha ya katikati hadi kuwa dereva taksi nilimficha kwa manaa yana ukakasi mkubwa sana pale atakapo yasikia.



“Siri gani hiyo mume wangu?”

Mke angu aliniuliza huku akinitazama machoni mwangu kwa umakini sana. Nikaa kimya kwa sekunde kadha kisha nikaendelea kuzungumza.

“Tulipelekwa kwenye kambi hiyo na tulianza kupatiwa mafunzo ya kijeshi ambayo sio ya kawaida na wanayo pewa wanajeshi hawa wa kawaida”

“Mmmm sasa una taka kuniambia mume wangu kwamba wewe ulikuwa ni mwanajeshi?”

Mke wangu aliniuliza kwa sauti ya upole sana.

“Yaa tulikuwa tuna pewa mafunzo magumu, mafunzo ya kuwa na roho mbaya, mafunzo ya kuua, mafunzo ya kuto jali binadamu mwengine. Kiufupi tulikuwa ni binadamu ambao ni kama mbwa wakali sana.”

“Mmmm mume wangu hiyo ni movie au ni maisha halisi kwa maana ume sema mulikuwa kama mbwa wakali, ila wewe mbona ni mpole, mstarabu na kama unacho kizungumza sio kweli vile?”

Nikatabasamu kidogo huku nikimtazama.

“Mke wangu niliweza kubadilisha maisha yangu mara baada ya rafiki zangu hao watatu kuuwawa kinyama sana”

Mke wangu akakurupuka na kukaa kitako huku akinitazama usoni mwangu kwa mshangao.

“Una taka kuniambia hao rafiki zako wame kufa”

“Sasa ni mwaka wanne toka wafe”

“Walikufaje kufajae?”

Mke wangu aliniuliza huku akionyesha dhairi kwamba amejawa na mshangao.

“Ngoja kwanza tuna kwenda taratibu uta elewa kila kitu. Katika hii nchi kuna vitengo vya kiusalama ambavyo vina julikana kama jeshi lapolisi, wanajeshi na kadhalika. Ila kuna vikosi maalumu ambavyo huwa havijulikani hivyo huwa vina itwa silaha ya siri ya serikali ambavyo huto weza kuwaona au hata kuzisikia ofisi zao sehemu zilipo”

Nikaa kimya kwa sekunde kadha akisha nikaendelea kuzungumza”

“Hivyo mimi na rafiki zangu tulipatiwa mafunzo kwa miaka minne mfululizo kabla ya kuanza kazi ramsi na tuliweza kupelelekwa katika nchi nane kufanya mazoezi ya kujiendelea katika kipindi hicho cha miaka minne”

“Baada ya hapo tukaingia katika kazi maalumu za kiserikali, ambazo tuliweza kuzifanya kwa ufahasaha mkubwa sana. Sifa zetu ziliweza kuene duniani kote hadi uumoja wa mataifa uka tuchukua na huko ndipo wezangu walipo uwawa”

“Sasa ilikuwaje ukawa dereva taksi?”

“Baada ya wezangu kuuwawa niliacha kazi kwa maana hapakuwa na umuhimu wa mimi kuendelea kufanya kazi na isitoshe nikaona ni kama vile Mungu amenipa nafasi nyingine ya kuweza kuishi na kuwa mume na baba bora katika familia nitayo ianzisha”

Mke wangu akakaa kimya huku akionekana kutafakari jambo fulani.

“Pole mume wangu kwa kuwapoteza wezako”

“Asante mke wangu nimesha poa.”

“Kipindi cha nyuma nilisha wahi kusikia kikundi kimoja cha wapiganaji hodari nchini Tanzania kinacho itwa X sasa miaka ya hivi karibuni kime kaa kimya sijajua wapo wapi?”

Nikatabasamu huku nikimtazama mke wangu kwa maana ni kweli kwa kipindi cha nyuma kikundi chetu cha X kilikua maarufu sana kwenye masikio ya watu wengi ila kitu ambacho kiliwachanganya wananchi wengi ni kwamba hawakuwahi kuwatambua watu wanao husika kwenye hicho kikundi ni kina nani kwa maana katika ufanyaji wa kazi zetu tulilikuwa tuna zifunika nyoso zetu kwa vinyago maalumu wa chumba ambavyo vyote viliweza kufanana. Tuliweza kusifiwa kwa kuzisaidia nchi nyingi za Afrika kupambana na vikundi sugu vya kigaidi kama Al-Shabab, Boko haramu na kadhalika.

“Ulisikia wapi hizo sifa za hicho kikundi?”

“Kwenye tv, redio magazetu. Kwani wewe ulikuwa huwajui?”

“Nina wajua na kiongozi wa kikundi hicho cha X nilikuwa ni mimi”

“Weeeee acha uongo Eddy. Hahaaaaa”

Mke wangu alicheka sana huku akinitazama usoni mwangu.

“Baby una nidanganya bwana, wale jamaa ni kiboko. Yaani ukisikia X ni X kweli mume wangu, jamaa walikuwa wakipambana kweli wana pambana walikuwa ni wanaume wa shoka”

“Kwa hiyo mke wangu huamini ninacho kuambia?”

“Ahaa siamini kwa kweli. Mume wangu wewe ni wakawaida sana, yaani sija wahi kukufikiria wala kukudhania kwamba una weza kuwa hata wanajeshi wa kawaida”

Nikatabasamu kwa maana kuto kuniamini kwa mke wangu, kume nipunguzia mzigo wa kumueleza hata mambo ambayo hakupaswa kuyasikia. Nikaanza kumchokoza kwa kumpapasa maeneo kadhaa ya mwili wake na kumfanya aanze kulainika na kunipokea taratibu na tukaanza kwenda mzunguko wa pili ambao pambano lake ni kali kuliko pambano la kwanza. Hadi tuna maliza mke wangu aka niomba apumzike kwa maana siku ya leo kuanzia asubuhi ilikuwa ni ndefu sana kwa upande wetu kwa maana mishe mishe za harusi sio jambo dogo.

Alfajiri na mapema nikawa wa kwanza kuamka, nikamuamsha mke wangu, tukajiandaa na kuianza safari ya kueleka ikulu. Hadi tuna fika kwenye geti la ikulu mke wangu bado akawa haamini kama kweli leo hii ana ingia katika jengo linalo lindwa kuliko majengo yote Tanzania. Tukatoa vitambulisho vyetu na baada ya kukaguliwa tukaruhusia kuingia ndani. Taratibu nikasimamisha gari hili lililo letwa hotelini na dereva wa makamu wa raisi, eneo la maegesho ya magari hapa ikulu. Tukashuka na mke wangu huku akishangaa shanga uzuri wa jengo hili la ikulu.

“Waooo ni pazuri sana mume wangu”

“Yaa twende ndani”

Tukaingia ndani huku wafanyakazi wanao nitambua wakinisalimia kwa furaha sana kwani ni miaka mitatu sija kanyaga katika jengo hili.

“Huyu ni mke wangu ana itwa Cauther”

Nilimtambulisha mke wangu kwa mzee mmoja ambaye ndio msemaji wa ikulu.

“Waoo hongera sana Eddy nilipata habari kwamba una funga ndoa sema mambo yaliingiliana nikashindwa kuudhuria”

“Usijali mzee wangu. Jambo la kumshukuru Mungu ni kwamba kila kiti kime kwenda vizuri”

“Makamu wa raisi ameniagiza kwamba ukifika nikupeleke moja kwa moja katika commanding room”

“Sawa mke wangu ana weza kupatiwa eneo la kupumzika?”

“Bila shaka”

Tukaongozana na mzee huyo pamoja na mke wangu hadi katika eneo la mapumziko.

“Mke wangu nina kuja nina kuomba sana uweze kunisubiria hapa. Ukihitaji chochote, waulize wale wadada wa kike pale wata kuhudumia”

“Sawa mume wangu. Kuna kitu sasa nina anza kukuamini”

Mke wangu alininong’oneza sikioni mwangu.

“Kitu gani?”

“Watu wana kuheshimu na kukujua. Au wewe ndio X kweli nini?”

“Sio mimi bwana mke wangu. Baadae”

Nikamnyonya denda mke wangu kidogo kisha nikaongozana na mzee huyu hadi kwenye ukumbi maalumu ambapo oparesheni zote za kiusalama zinazo endela ndani ya ikulu zina fanyika humo. Baadhi ya wafanyakazi wanao nifahamu wakanisalimia kwa mbali mbali kwa maana nime fanya nao kazi kwa kipindi kirefu huku wengine wakiwa wana nishangaa kwa maana ndio kwanza wana niona leo. Nikasalimiana na makamu wa raisi kisha akanikaribisha kwenye kiti huku nikitazamana na wakuu wa jeshi wa ngazi za juu sana walio hudhuria kwenye kikao hichi.

“X nina imani kwamba upo tayari kwa kazi?”

Makamu wa raisi aliniulza huku akinitazama usoni mwangu

“Ndio maana nipo hapa mkuu”

“Safi. Tume kuandalia timu ya vijana wawili ni makomandoo kutoka jeshi la ulinzi wa taifa. Wa kwanza ana itwa Maulid na wapili ana itwa Judithi. Wamesha jiandaa kwa ajili ya kazi hii. Tumeweza kugundua kwamba ndege bado ipo nchini Sudan katika mji wa Nzara na eneo hilo ndipo magaidi walipo iweka ndege ya raisi pamoja na mateka wote wapo eneo hilo.”

Makamu wa raisi alizungumza huku ramani ya eneo hilo ikionekana kwenye tv kubwa iliyopo katika ukumbi huu.

“So X uta ongoza oparesheni hii ukiambatana na vijana hawa wawili”

“Uwezo wao upo vipi?”

“Wamepitia mfunzo yote na hadi wamehitimu kuwa makomandoo ina maana wapo vizuri”

Mkuu wa majeshi alizungumza kwa kujiamini huku akinikazia macho.

“Sawa, oparesheni mume panga ianze saa gapi?”

“Saa tatu kamili muta ondoka hapa na ndege ya jeshi”

Nikaitazama saa yangu ya mkononi ina nionyesha ni saa mbili kasoro asubuhi.

“Poa muheshimiwa, nina imani sina cha kusikiliza zaidi si ndio?”

“Je utahitaji kufahamu details za wezako unao ambatana nao?”

“Hapana, mkuu wao amesha nidhibitishia kwamba wapo vizuri. Sifa za maneno hazisaidi kwenye uwanja wa vita ila vitendo ndio kila kitu. Mkuu tafadhali kama ita wezekana nina weza kuzungumza nawe kidogo”

“Hakuna shaka”

Wakuu hawa wa majeshi wakanitazama kwa macho makali kwa maana nina wafahamu vizuri ni watu ambao siku zote walikuwa wakichukia kundi langu la X kwa maana vijana wao walikuwa hawafui dafu mbele yetu.

“Ndio X”

Makamu wa raisi alizugumza huku akiwa amesimama na mimi pembeni kidogo.

“Naomba nikakutambulishe kwa mke wangu”

Makamu wa raisi akaitazama saa yake ya mkononi.

“Una dakika tano”

“Shukrani mkuu”

Tukatoka katika ukumbi huu ulipo chini ya ardhi katika eneo hilo la ikulu. Tukaingia katika eneo alipo kaa mke wangu na alipo tuona mimi na makamu wa raisi akasimama na akamsalimia makamu wa raisi kwa heshima kubwa sana huku akiwa haamini anacho kiona.

“Mke wangu ana itwa Cauther”

“Nashukuru kukufahamu binti yangu na hongera sana kwa kuingia katika familia ya mwanangu”

“Nina shukuru”

“Jana nilipo muambia kwamba nime onana na makamu wa raisi hakuamini. Ila sasa nina hisi ata kuwa ameamini.”

“Ni kweli ilikuwa ni ngumu kuamini muheshimiwa”

“Wewe niite baba usiniite muheshimiwa kwa maana X hapa ohoo samahani Eddy ni kijana wangu nimemlea mimi mwenyewe”

Makamu wa raisi alijichanganya mbele ya mke wangu na kuniita jina la X na kumfanya mke wangu azidi kuamini kile nilicho mueleza usiku japo alikuwa ana hisi ni kama simulizi ya filamu vile.

“Nashukuru sana baba”

“Asante. Pia nisamehe bwana kwa kumuiba mume wako katika usiku wa jana nina imani ulijawa na hofu?”

“Hakuna shaka”

“Mke wangu, chochote utakacho hitaji, mzee ata kupatia hapa nina siku kama mbili hivi sinto kuwepo ndani ya Tanzania”

Mke wangu akanitazama kwa mshangao kidogo.

“Acha niwaache muzungumze. Ukimaliza uta onana na rubani”

“Sawa mkuu”

Makamu wa raisi akaondoka na akaniacha na mke wangu.

“Baby usiniambie ulicho zungumza jana ni kweli?”

Mke wangu alizungumza huku akinikazia macho.

“Ndio mke wangu?”

“So una niacha peke yangu ikiwa hata honeymoon yetu haijaisha?”

Cauther alizungumza kwa kufoka kidogo jambo ambalo nilisha litambua mapema.

“Mke wangu kuna kitu muhimu nina kwenda kukifanya”

“Kitu gani, kwa nini hujanieleza siku zote una kuja kuniambia hapa ikulu, ehee?”

Cauther akazidi kufoka kiasi cha kunifanya nikae kimya kwa sekunde kadhaa huku nikimtazama jinsi uso wake ulivyo jawa na hasira na furaha yote imesha mpotea. Taratibu nikamvuta kifuani mwangu na kumkumbatia kwa nguvu na kumfanya aanze kulia.

“Nilihisi kwamba uta kuwa nami kila siku kwenye maisha yangu. Ila kwa nini una niacha peke yangu mume wangu”

Cauther akaendelea kulalamika huku akilia kwa uchungu sana.

“Mke wangu hii kazi ni ya muhimu sana na nilifanya kuombwa sana kwa maana nilisha kataa kuifanya”

“Ohoo kwa hiyo ukakubali na kuona mimi sina umuhimu si ndio?”

“Sio hivyo mke wangu?”

“Ila?”

“Raisi na ndege yake wame tekwa. Hapa unavyo ona ni kwamba nchi ina ongozwa na makamu wa raisi. Walinzi wa raisi pamoja na wafanyakazi alio ambatana nao wana uwawa kila baada ya lisaa moja na magaidi hao hivyo nina kwenda kumrudisha raisi nyumbani tu alafu nina achana na mambo hayo na tuta kwenda kuishi mbali mke wangu”

Nilizungumza huku nikimtazama mke wangu machoni. Tukatazamana kwa sekunde kadhaa.

“Ulicho ongea ni kweli baby?”

Mke wangu alizungumza kwa kudeka kidogo.

“Ndio ni kweli ndio maana makamu wa raisi aliweza kunifwata jana. Zile sifa za kundi la X ulizo kuwa una zisikia basi mimi ndio kiongozi wao”

Cauther akashusha pumzi nyingi na taratibu nikaanza kumfuta machozi usoni mwake.

“Kama kweli wewe ni X nahitaji unihakikishie kwamba una mrudisha raisi Tanzania”

Mke wangu alizungumza huku akiachia tabasamu pana lililo nipa nguvu mpya na amani moyoni mwangu.

“Usijali mke wangu nita fanya hivyo”

“Nina kusubiria na urudi ukiwa hai”

“Asante mke wangu”

“Ila niahidi kwamba hii ni kazi ya mwisho?”

“Ndio ni ya mwisho sinto fanya tena”

“I love you Eddy”

“I love you too my wife”

Tukaanza kunyonyana denda na mke wangu, hatukujali wafanyakazi walipo eneo hili. Tulipo ridhika tukaachiana, mke wangu taratibu akavua cheni ambayo nilimpa kipindi kirefu tulivyo kuwa tume anza mapenzi yetu.

“Toka ulivyo nivisha ile siku, sikuwahi kuivua hadi leo hii ndio nime ivua. Nakuvisha nahitaji urudi ukiwa salama mume wangu”

Cauther alizugumza huku taratibu akinivisha cheni hiyo.

“Nita rudi salama”

Nikakumbatiana na mke wangu kwa mara nyingine kisha tukaachiana.

“Mungu akutangulie mume wangu”

“Amen”

Nikaondoka eneo hili huku nikimuacha mke wangu akinisindikiza na macho yaliyo jaa huzuni. Nikakutana na rubani wa helicopter ya ikulu.

“X helicopter ipo tayari”

“Poa”

Tukaelekea katika kiwanja kidogo cha helicopter tukapanda helicopter hiyo na moja kwa moja tukaelekea katika kambi ya jeshi la anga. Nikashuka kwenye helicopter na nikapokelea na mkuu wa kambi hiyo.

“Una dakika thelathini za kujindaa hakikisha una fanya haraka”

Mkuu wa kambi hii alizungumza kwa suati ya juu, hii ni kutokana na milio mikubwa ya ndege za kijeshi zinazo paa na kutua.

“Rogue that”

Nilizungumza huku nikitembea kwa mwendo wa haraka hadi kwenye chumba maalumu cha maandalizi. Nikawakuta vijana wawili mmoja wa kike na mwengine wa kiume wakiwa tayari wamesha jiandaa.

“Nyinyi ni kina nani?”

Niliwauliza huku nikiwatazama kuanzia chini hadi juu.

“Mimi ni Maulid”

“Mimi ni Judy”

“Okay nyinyi ndio makomandoo nilio ambiwa?”

“Ndio”

Nikawatazama kwa dakika mbili pasipo kuwasemesha chochote, nikatambua wana mapungufu makubwa.

“Muna familia, mke, mume au watoto?”

“Ahaa mimi sija olewa, ila nina bibi na babu wazazi wangu wamesha fariki”

“Na wewe je?”

“Mimi nina mtoto mmoja pamoja na mama mzazi ila sija oa bado”

“Mume shawahi kwenda kwenye oparesheni yoyote kubwa?”

“Hapana hii ndio mara yetu ya kwanza kwa maana tume hitimu mafunzo ya ukuomandoo miezi sita iliyo pita”

“Ohoo Mungu wangu. Sikilizeni, nyinyi ni wadogo zangu. Huko tunapo kwenda kuna kufa na kupona. Muna nafasi ya kuendelea kuishi kama una jihisi ulichaguliwa kwa kulazishwa basi niambie mimi nita liripoti hili na muta baki na nita kwenda peke yangu”

Maulid na Judy wakatazamana. Ishara hiyo ikanidhihirishia kuna kamsukumo ka kulazimishwa kame wapiti.

“Sikilizeni hamuna haja ya kuandamana nami. Hivyo muna weza kurudi kambini”

“Ila sisi ni makomandoo na tupo tayari kwa lolote”

Maulid alizungumza kwa kujiamini huku akinitazama kwa macho ya ukakamavu.

“Komandoo ni mtu mzuri ila si kwa kazi hii tunayo iendea wadogo zangu. Mupo tayari kwa lolote si ndio?”

“Ndio mkuu”

Walizungumza kwa kujikaza. Nikawatizama kwa dakika kadhaa kisha nikavua saa yangu na kuitazama, nika seti dakika tano.

“Muna dakika tano za kunishambulia mukifaulu kuni mudu basi muna kwenda mukishindwa muna baki tume elewana?”

Maulid na Judy wakabaki wakiwa wamebung’aa kwa mshangao. Nikaruka hewani na kujizungusha kwa kasi ya ajabu na kurusha teke alimaarufu round kick ambalo likatua kifuani mwa Maulid aliye valia jaketi la kuzuia risasi, uzito na nguvu la teke hilo likamuangusha chini Maulid kama gunia na kumfanya Judy kushangaa kwa maana hakutarajia kuona mwezake akiaguka kwa mfumo mzima mzima pasipo hata kujisaidia yeye mwenyewe.



“Pigana”

Nilizungumza huku nikimtazama Judy usoni mwake. Akakaanza kurusha ngumi na mateke huku akinikabidi kwa kasi sana. Ila kasi yake nikawaze kuihimili na kurudisha mashambulizi kadhaa yaliyo muangusha chini. Maulid naye akasimama na kuanza kunishambulia. Mkuu wa kambi hii akaingia ndani hapa na akajawa na mashangao.

“Ni upumbavu gani unao endelea humu ndani?”

“Nina wapima vijana”

Hadi dakika tano zina kwisha Judy na Maulid kidogo wakawa wamejitahidi kuto kushindwa.

“Kazi nzuri vijana”

Nilizungumza huku nikivua nguo zangu. Nikabakiwa na boksa na kuingia bafuni, nikagoga haraka haraka na kutoka huku nikiwa nimejifunga taulo.

“X una matatizo gani?”

Mkuu wa kambi alimuliza.

“Kwa nini?”

“Kuwapima vijana ni hadi upigane nao?”

“Uta juaje wana weza kuwa ndio ma X wafwatao. Mzee hii ni kazi yangu ya mwisho kwa serikali, baada ya hapo nina stape down mazima. Yaani hata aje nani kuniomba sinto mkubalia”

“Jiandae bwana muda ume kwisha.”

Nikasimama eneo zilipo kombati za jeshi, nikazitazama kwa dakika mbili huku nikikumbuka miaka ya nyuma siku yangu ya kwanza kupewa kombati la jeshi na kulivaa, ilikuwa ni siku ambayo nilijawa na furaha sana. Siku ambayo nilijiona kwamba ni mtu maalumu sana hapa duniani. Nikachukua surualia mbayo ina nitosha na kuivaa. Nikafwatia tisheti ya blue, kisha nikamalizia na shati zito kidogo. Nikavaa buti nyeusi, nikamaliza kujiandaa kisha nikasimama kwenye kabati lenye silaha. Nikachukua bastola nne aina ya M17 zilizo jaa risasi. Mbili nikazichomeka kiunoni huku mbili nikizichomeka katika mguu wa kulia na mguu wa kushoto. Nikavaa jaketi la kuzuia risasi nikachukua bunduki mbili moja ikiwa ni MP5 na nyingine ni MK 20 SSR. Nikachukua mabomu manne ya kurusha kwa mkono ambayo ni M67 Fragmentation Granade na mabomu mawili aina ya M18 smoke grenade.

“Madogo are we good?”

“Yeah boss”

Judy na Maulid walizungumza kwa furaha sana. Nikaitazama pete aliyo nivisha mke wangu siku ya jana kanisa, nikataka kuivua ila nikagairi. NIkachukua gloves ngumu na kuzivaa,

“Mkuu nahitaji kumtumia mke wangu selfie yangu”

Nilizungumza huku nikichukua simu yangu kwenye mfuko wa suruali niliyo ivaa. Nikapiga selfie kadhaa kisha nikazituma kwa mke wangu. Haikuisha hata dakika moja mke wangu akanipigia video call.

“X muda una kimbia”

“Dakika moja mkuu”

Nilizungumza huku nikipokea video call hiyo.

“Hei baby”

“Woo mume wangu you look so nice”

“Asante mke wangu. Ume amini ehee?”

“Yeah nimeamini. Make sure una rudi salama”

“Don’t worry baby”

“I love you”

“I love you too”

Mke wangu akanibusu na nikakata simu na kuirudisha kwenye mfuko wa suruali yangu niliyo jia hapa kambini. Tukatoka katika chumba hichi na kuelekea ilipo ndege inayo tusubiria.

“X ni lini ume oa?”

Mkuu wa kambi aliniuliza.

“Jana mkuu”

“What?”

“Yea ni jana tu”

“Hongera sana”

“Nashukuru”

“Nahitaji uwalinde na kuwaongoza hawa vijana”

“Rogue that boss”

Mkuu wa kambi akatuaga kwa kutupa mikono na taratibu tukaingia kwenye ndege hii kubwa aina ya C17A Globemaster III. Tukaa kwenye siti maalumu za kurazamana na kufunga mikanda na taratibu ndege hii ikaanza kupaa angani. Ilipo kaa sawa nikafungua mkanda wa siti na kusimama. Nikasalimiana na wanajeshi wawili tulio wakuta humu ndani

“Karibu sana X”

“Shukrani sana”

“Vipi ume ndio ume rudi kazini mazima au?”

“Hapana ni kazi hii tu”

“Sawa ndugu yangu. Sisi bado tuna endelea kuwajibika”

“Ndio maisha tuliyo yachagua.”

“Hahhaa haya bwana. Tusikilizane”

Mwanajeshi huyu alizungumza huku akiwatazama Judy pamoja na Maulid.

“Hizi ni kofia ngumu, zime unganishwa na kamera pamoja na earphone ya mawasiliano. Kila kitakacho kuwa kina fanyika katika oparesheni yenu kina onekana ikulu pamoja kita sikika pia ikulu.”

Mwanajeshi huyu alizungumza huku akituonyesha kofia hiyo inayo itwa liberator v advanced dual communications headseat. Kila mmoja akakabidhiwa kofia yake na iliyo tengezwa kwa chuma na hata ukipigwa risasi ya kichwa basi sio rahisi kupenya. Tukapewa mabegi ya parachute pamoja na miwani zitakazo tusaida kuruka umbali mrefuku kutoka ardhini.

“Muna masaa matano kuanzi hivi sasa ya kupumzika”

Mwanajeshi huyu alizunngumza mara baada ya kila mtu kuvaa begi hilo.

“Mkuu”

Judy alinita huku akiwa amekaa pembeni yangu.

“Naam”

“Kwa nini ulitupa mtihani wa kupambana na wewe?”

Nikatabasamu huku nikimtazama usoni mwake.

“Kwa sababu eneo tunalo kwenda hatuendi kupambana na mtu mmoja. Ni kikundi au niseheme ni jeshi la waasi ambalo ndio lime mteka raisi wetu. Hivyo wata kuwa wapo full treining kuanzia kwenye matumizi ya silaha hadi kwenye matumizi ya mikono na miguu. So ina bidi mujiandae kwa jambo lolote lile litakalo tokea mbele yetu. Tume elewana?”

“Ahaa sawa mkuu. Je nina weza kuuliza ni kwa nini una itwa X?”

Swali la Judy likanifanya nikae kimya kwa dakika mbili.

“Nime sahau kisu”

Nilizungumza na mwanajeshi mmoja ambaye alikuwa ana tupatia maelekezo akanipatia kisu aina ya D80 NK-123.

“Dogo ume nipatia sana.Ume juaje nina penda kutumia hichi kisu”

“Nina kujulia kaka”

“Safi mdogo wangu”

Nilizungumza huku nikimtazama mwanajeshi huyu aliye nipatia kisu hichi. Nikasoma jina lake katika combati yake aliyo vaa eneo la mfuko wa shati hilo na kutambua jina lake ana itwa Richard W.D.

“Ehee Judy nina rudi kwenye swali lako”

Nilizungumza huku nikikichomeka kisu hichi kwenye moja ya mfuko wa suruali niliyo ivaa.

“X ni kikosi maalumu ambacho kilitengenezwa mahususi kwa ajili ya kupambana na matukio makubwa sana ya kiuhalifu hususani ya kigaidi.

“Katika timu yetu tulikuwa ni wanajeshi wanne tu ambao sisi sote umri wetu ulikuwa ni mmoja na tulikuwa ni atu ambao tulikua pamoja. Tuliingia jeshini tukapatia mafunzo, tukavuka levo yenu ya ukomandoo, tukapewa mafunzo mengi mengi sana ambayo yalituganya tuwe ni zaidi ya makomandoo wa kawaida. Tuliweza kupambana na vikundi vingi sana vya magaidi. Ila nina kumbuka siku moja tulifanyiwa ambush ambayo ilisababisha wezangu watatu kufariki huku nikisalia mimi mwenyewe”

“Ilikuwaje hadi mukafanyiwa ambush?”

Nikakaa kimya huku picha kamili ya tukio zima lilivyo tokea nchini Pakistani katika eneo Bajour eneo ambalo lina milikiwa na kundi la kigaidi la Teleban.

“Dogo”

“Ndio mkuu”

“Umesha wahi kushuhudia magaidi wenye roho mbaya?”

“Kwa nini una niuliza hivyo mkuu?”

“Kwa sababu katika maisha hakuna kitu kibaya kama binadamu mwenzako akiwa ameshika silaha. Tulikuwa tupo na vikosi vya umoja wa mataifa pamoja na wanajeshi wa Pakistani. Ule mji ulikuwa una shikiliwa na kikundi cha kigaidi cha Taliban. Tukiwa njiani tuna elekea katika mji huo, sijui ni nani ambaye alichomesha siri ya kwamba tuna kwenda kuvamia. Tuliweza kufanyiwa ambushi babu kubwa. Katika siku za maisha yangu siku ambazo nilipiga risasi nyingi ni siku hiyo. Wale jamaa walikuwa ni wengi na isitoshe sisi tulikuwa tuna pita kwa chini na wapo wapo milimani. Usiombee mdogo wangu upigwe kutokea juu.”

“Pole mkuu”

“Nimesha poa.”

“Uliokokaje kaka”

Maulid aliniuliza.

“Ahaa unajua mimi nilikuwa kwenye gari nyingine na wanajeshi kutoka Marekani, wezangu walikuwa katika gari nyingine kwa maana tuliongozana kama gari kumi na tano hivi zilizo jaa wanajeshi. Mbaya ilikuwa ni usiku kwa maana tulikuwa tuna panga kwenda kuwavamia kwenye milima yao. Ila kwa haraka haraka nina hisi kuna mpuuzi aliweza kuchomesha siri hiyo kwa maana halikuwa jambo rahisi kwa magaidi kuweza kujua”

“Muna muhisi ni nani?”

Richard aliuliza.

“Ni ngumu sana kujua mukiwa muna fanya kazi mataifa zaidi ya kumi katika jeshi moja. Na wala sihitaji kufwatilia hili jambo kwa maana lita nipa maumivu. Mwezetu mmoja alikua kwenye gari lililo shambuliwa kwa bomu, wengine walikufa kwa riasi nabomu. Mimi nilijeruhiwa risasi ya paja la mguu wa kulia. Uzuri iliingia na kutokea upande wa pili. Kwenye ile milima kuna maeneo mengi sana ambayo niliweza kujibanza hadi varangi lilivyo isha huku nikishuhudia wezangu wakikatwa vichwa na vikachomekwa kwenye miti iliyo chongeshwa na kupelekwa kwenye kambi zao”

“Masikini pole sana mkuu”

Judy alizungumza kwa sauti ya masikitiko.

“Nashukuru, nilikaa pale kwa siku mbili mfululizo huku nikiwa sina chakula sina risasi, nilicho kuwa nime bakiwa nacho ni kisu tu cha aina hii ambayo kiliweza kunisaidia kuishi kayika misitu ile”

“Kilikusaidiaje?”

“Nilikuwa nina kula magome ya miti huku nikitafuta eneo ambalo nina weza kupata msaada. Nashukuru Mungu nifanikiwa kukutana na mabinti fulani hivi wakiwa kwenye kama bwawa wakichota maji. Hiyo ilikuwa ni siku kama ya tano hivi porini. Kitu kilicho weza kunisaidia ni kwamba nikikuwa nina jua lugha yao hivyo niliwaomba msaada na nikwaeleza kwamba mimi ni mtu mzuri. Wakanipeleka katika mapango yao waliyo kuwa wamejificha na familia zao kwa maana wananchi walikuwa wana ogopa sana kuishi na magaidi hao hususani watoto wa kike kwa maana walikuwa wana nyenyeswa kingono na mambo mengine”

“Aisee”

“Yaa munajua Tanzania kuna amani sana. Nchi hii haina keshi keshi nyingi hata nyinyi wanajeshi wa kawaida muna ishi kwa furaha sana. Ila usiombee kwenda kufanya oparesheni kama hizo, ukirudi salama, acha kwenda hususani ukiona shambulizi kama lililo wakuta ndugu zangu.”

“Daa pole sana kaka”

“Nina shukuru.”

“Sasa baada ya kuhudumiwa na wale wadada ikawaje?”

Maulid aliniuliza tena.

“Nilikaa kwenye mapango hayo kwa miezi kama mitatu huku nikijaribu kutafuta njia ya kuondoka katika mji huo kwa maana ulikuwa ume shikwa na magaidi hao kiasi kwamba hapakuwa na njia rahisi ya kuweza kutoka.”

“Katika wale mabinti kuna kaka yao mmoja naye alikuwa ana fanya kazi kwenye kundi hilo la magaidi. Ila alikuwa sio mtu mmbaya kwa maana vijana wa kiume walikuwa wana ingizwa kwenye jeshi hilo la magaidi kwa kushinikizwa, yaani utake usitake uta kuwa mwanajeshi wao na ukikataa wana kuua wewe na familia yako”

“Jamaa alikuwa ana kuja kuwatembelea kwa siri sana familia yake. Mdogo wake alimueleza juu ya haja yangu ya kutoka katika kambi hiyo hivyo jamaa aliweza kunisaidia kwa moyo mmoja. Alinipitisha njia za siri na nikafanikiwa kutoka katika mji huo na moja kwa moja nikaelekea katika ubalozi wa Marekani, nikaoelekwa makao makuu ya umoja wa mataifa na nikarudi nchini Tanzania na kuazia hapo nika achana kabisa na kazi ya jeshi na ilibidi nikae mwaka mzima nikifanyiwa matibabu ya kisaikolojia”

“Yaa kwa matukio kama hayo ni lazima uathirike kisaikolojia”

Richard aliniunga mkono.

“Aise pole sana. Una jua sifa za kikundi chenu cha X ndio kilicho nivutia sana mimi kujiunga na jeshi”

Judy alizungumza huku akinitazama usoni.

“Kweli?”

“Ndio na nilimuuliza mmoja wa wakufunzi wangu juu ya kikundi hicho, akaniambia kwamba kilisha potea ila hakuweza kunitajia ni kina nani wahusika”

“Yaa lilikuwa ni pigo kwa serikali ya Tanzania kwa maana tulikuwa ni human weapon. Yaani tulikuwa hatushindwi na jambo ila ya Mungu mengi bwana, siku ikifika ime fika kwa maana katika wanajeshi themanini na sita tulio kuwa katika ule msafara ni mimi peke yangu ndio nilikuwa nime baki ila wengine wote walikufa”

“Aisee”

“Yaa ndio maana nalijifikiria sana kuifanya hii kazi. Laiti ingekuwa sio makamu wa raisi nisinge thubutu kunyanyua mguu wangu kwenda kwenye hii oparesheni. Ila tuachane na hayo, nina omba ramani”

Ilibidi nipotezee mada hiyo kwa maana nina weza kuwapa hofu Mulid na Judy. Richard akanikabidhi ramani ya eneo tunalo kwenda.

“Mumesha pitia hii ramani?”

“Ndio mkuu”

“Ndege ya raisi ipo eneo hilo according na picha za settelaite. Katika eneo hili kuna msiti pamoja na uwanja mkubwa ambapo ndipo ndege ilipo. Magaidi wa eneo hilo wana watumia hadi vijana wadogo sana katika maswala ya kijeshi hivyo ina wapasa kuwa makini kwa maana musije muka muona mtoto muka hisi ni rafiki kwenu”

Richard alizungumza huku akinionyesha kwa kidole eneo hilo. Richard akatukabidhi simu maalumu za kijeshi ambazo zina tusaidia kutazama eneo maalumu alipo raisi kwa maana ana kifaa kidogo cha gprs kinacho muonyesha ni wapi alipo yeye na mke wake. Nikatazama ramani ya eneo hilo kwa umakini na kuyakremisha maeneo yote kwa umakini wa hali ya juu kisha nikamrudishia Richard ramani hiyo huku simu nikiingiza mfukoni. Tukafika katika anga la South Sudan, tukasimama na kujiandaa tayari kwa kuruka huku kila mmoja akiwa ameka miwani yake sawa pamoja bunduki yake sawa. Marubabi wakatutangazia kwamba muda wa kuruka sasa ume wadia. Taratibu eneo la nyuma la ndege hii likafunguka, nikawatazama Maulid na Judy na kuwapa ishara ya dole gumba. Tukawasha earphone zetu kwa ajili ya mawasiliano. Richard na wezake wakatupa mikono ya kutuaga kisha Maulid akawa wa kwanza kuruka, huku akifwatia Judy kisha nikafwatia mimi. Nikaitanu miguu na mikono yangu hewani huku nikiwa nime tumbo na uso wangu vikielekea chini. Nikawaona Judy na Maulid nao wakiwa katika mfumo huo. Nikajigeuza na kutanguliza kichwa chini huku miguu na mikono nikiwa nime ibana na kunifanya nizidi kwenda kasi kuelekea chini. Nilipo ridhika nime fika mita kadhaa, nikafungua parachute langu na nikaanza kuelea hewani. Nikaanza kushuka taratibu na kufanikiwa kukanyaga ardhi ya nchi hii ya Sudan Kusini. Nikavua begi langu la parachute na kulikunja kwa haraka parachute hili na kulificha kwenye moja ya kichaka.

“Hei”

Niliwaita Mulid na Judy kwa maana nime tua sehemu tofauti na wao.

“Mau na Judy muna nisikia?”

Niliita kwa sauti ya chini huku nikiwa nimesha shika bundiki yangu, huku bunduki ambayo ni sniper nikiwa nime ivaa mgongoni mwangu. Ukimya wao ukanipa wasiwasi sana, nikatoa simu hii na kutazama eneo ambalo nipo mimi kwa maana ina saidia kuonyesha location zetu sisi watatu. Nikawaona Maulid na Judy wakiwa upande wangu wa kaskazini. Nikaanza kukimbia kuelekea eneo hilo na halikuwa mbali sana na nilipo. Nikasikia kelele za wanajeshi wakishangilia. Nikajibaza kwenye moja ya kichaka, sikuamini macho yangu mara baada ya kuwaona Judy na Maulid wakichezea kipondo kikali kutoka kwa wanajeshi walio wazunguka wakiwa na silaha za kila aina na asilimia sabini ya wanajeshi hao ni vijana chini ya miaka kumi na nane.



“Ndio maana sikuhitaji hawa watoto waje”

Nilizungumza kwa hasira huku nikijaribu kutafakari ni nini cha kufanya kwa haraka kwa maana nikiwaacha hawa vijana wana weza kuuwawa huku nikiwashuhudia.

“X unanisikia?”

Niliisikia sauti ya makamu wa raisi kupitia headphone nilizo zivaa.

“Ndio mkuu “

“Mission ni kumuokoa raisi na watu wake ukiwasaidia hao wata fahamu kuna uvamizi. Hivyo muokoe raisi na watu wake hilo ndio chaguo la kwanza”

Nikajifikiria kwa muda huku nikiwatazama jinsi Judy na Maulid wanavyo endelea kupokea kipigo hicho kitakatifu.

“Fuc**”

Nilizingumza huku nikikaza vizuri kiwambo cha kuzuia sauti ya risasi kwenye bunduki yangu. Nilipo hakikisha nipo vizuri. Nikawatazama wanajeshi hao, kwa kasi ya ajabu nikaanza kuwashambulia wanajeshi hao ambao wakajikuta wakitawanyika pasipo kujielewa. Judy na Maulid nao wakapata upenyo wa kujiokoa huku wakipambana vikali na wanajeshi hao. Japo roho ina niuma sana kumuua mtoto ila sina jinsi zaidi ya kuendelea kuwashambulia. Mapigano hayo yakadumu kwa dakika kumi na nikafanikiwa kuwau wanajeshi wote.

“Mupo vizuri?”

“Ndio mkuu”

Nikawatazama Judy na Maulid wanao vunjwa na damu kwenye nyuso zao kwa maana kipigo kilicho wapata sio cha mchezo mchezo.

“Uwezekano wa kumuokoa raisi ni mdogo sana. Hivyo tuharakishe”

Nilizungumza huku tukiondoka eneo hili. Judy na Maulid wakawa na kazi ya kutufwata kwa nyuma huku tukikimbia kwa kasi sana kuelekea katika eneo ambalo ndipo inapo soma alama ya kwamba raisi na mke wake wapo. Tukafika katika kambi moja kubwa sana na tukafanikiwa kuiona ndege ya raisi ikiwa ime zungukwa na anajeshi. Umbali wa kutoka eneo ambalo tuliwaua wanajeshi na hapa ilipo kambi hii ni kama kilomita tano na pointi zake.

“Ina onekana hawajastuka”

Judy alizungumza huku akiwa ana tazama kambi hiyo kwa kutimia darubini.

“Wale wanajeshi walikuwa na vyombo vyovyote vya mawasiliano?”

“Hapana walikuwa hawana hata simu ya upepo na ina onyesha ni local sana”

Nikatazama saa yangu na ina onyesha ni saa kumi na mbili usiku, kwani tume tumia masaa mawili na nusu kufika katika kambi hiyo.

“Mkuu ila katika hii kambi kuna wazungu”

Judy alizungumza huku akinikabidhi darubini yake. Nikaichukua darubihi hii na kutazama kinacho endelea katika hii kambi na kweli nikawaona wanajeshi wa kizungu ambao wapo pamoja na wanajeshi wa kiafrika. Nikawasha headphone yangu na kuanza kuwasiliana moja kwa moja na watu walipo ikulu. Maulid akafungua begi lake na kutoa kamera ya kuendesha kwa rimoti(drone) ambayo ni ndogo kiasi.

“Muheshimiwa makamu wa waisi una nisiki?”

“Ndio X nina kusikia”

“Drone sasa hivi ipo hewani je muna ona tunacho kiona sisi?”

Nilizungumza huku nikitazama katika simu anayo itumia Maulid katika kuendesha drone hiyo.

“Yaa tuna ona”

“Hao wanajeshi wa kizungu muna weza kuwatambua?”

“Dakika moja”

“X hatujaweza kuwatambua kabisa ni kina nani”

Makamu wa raisi alizungumza.

“Madogo sikilizeni. Nyinyi bakini hapa, mimi nina shuka na kuingia ndani ya hii kambi tume elewana?”

“Sawa mkuu”

Chochote kitakacho tokea, musije hadi muone nina toka na raisi”

“Sawa”

Nikaanza kuingia kwenye kambi hii kwa umakini wa hali ya juu sana. Kitu ambacho siku zote adui huwa ana jua kabisa kwamba mpinzani wake hawezi kukifanya ni kumvamia katika majira ambayo kuna mwanga. Hivyo hata ulinzi wa kambi hii haukuwa mkali sana kwa maana bado giza halijatawala anga. Nikazidi kujipenyeza kwa umakini sana hadi nikafanikiwa kufika eneo la karibu kabisa na ndega ya raisi. Ndege ya raisi ina lindwa na magaidi sita ambao wame izunguka.

“Mkuu kuwa makini”

Nilisikia sauti ya Maulid nyuma yangu”

“Usijali”

Nilizungumza huku nikitoa simu yangu ndogo mfukini. Nikaitazama alama mbili nyekundu na zina onyesha kwamba raisi, mke wake wapo ndani ya ndege hii.

“Judy”

“Ndio mkuu”

“Una wapata hawa magaidi?”

“Yee wapo kwenye target”

“Niondolee wawiliwa upande wa kulia hawa wengine nita shuhulika nao”

“Rogue that”

Nikawashuhudia walinzi wawili wakianguka chini kimya kimya kwa maana Judy ana bundiki yenye uwezo wa kulenga mbali(Sniper) Nikachoboa bastola yangu ya kiunoni na kuifunga kwa haraka kiwambo cha kuzuia sauti ya risasi. Nikawapiga risasi wanajeshi wawili walipo upande wangu na wakaanguka chini pasipo wezao kufahamu kwa maana hii ndege ya raisi ni kubwa sana Nikawavuta na kuwaficha eneo ambalo sio rahisi kwa wao kuonekana. Nikabingiria na kupita chini ya ndege hii na kutokea upande wa pili, nikachomoa nichomoa kisu na kumpiga kabari gaidi mmoja kwa nyuma, nikaivunja shingo yake mwenzake ambaye alikuwa ame mpa mgongo akageuka kwa haraka kumtazama mwenzake ila sikumpa nafasi ya kufanya chochote. Nikakirusha kisu na kikatua shingoni mwake na akaanguka chini. Nikamsogelea kwa haraka na kukichomoa kisu changu, nikawavuta na kuwaweka chini ya ndege.

“Clear”

Judy alizungumza na nikamsikia vizuri, neno lake lina maanisha kwamba hakuna gaidi yoyote aliyooo karibu na ndege ya raisi. Nikafungua mlango wa chini na wa siri katika ndege hii ya raisi na nika ingia kwa maana kama ninge tumia mlango wa kuingilia ndani ya ndege hii basi inge nigarimu sana kwa maan ni lazima nigetumia ngazi ndefu kwani ndege hii ni Airbus A380. Nikaufunga mlango huu wa siri na nikatokea eneo ambalo huifadhia mizigo.

“Nielekezeni ni wapi nina elekea?”

“Una tumia ramani ya ndege nzima”

Makamu wa raisi ambaye ana itazama oparesheni hii kutokea ikulu alizungumza. Nikatumia picha za ramani nzima ya ndege hii ya kifahari ambayo ndio ndege kubwa na ya garama inayo milikiwa na maraisi duniani. Nikaitazama ramani hii kwa muda kisha taratibu nikaanza kutafuta eneo ambalo nina weza kupata mlango wa kutokea eneo la abiria. Nikafanikiwa kutokea eneo la abiria. Nikafungua mlango huu taratibu, nikachungulia na nikafanikiwa kuona eneo hili likiwa wazi”

Taratibu nikapanda ngazi na kuingia eneo la juu. Nikaufunga mlango huu huku nikiwa nina bastola yangu yenye kiwambo cha kuzuia sauti, mkononi. Nikaanza kuifwata kordo ndefu. Nikafika kwenye moja ya chumba, nikafungua taratibu na kukuta maiti za wafanyakazi wa wili wa kike wa ndege hii, ambao wame uwawa kwa kuchomwa visu huku nguo zao zikiwa zime chanwa chanwa na ina ashiria kwamba walibakwa kabla ya kuuwa.

“X umefanikiwa kumuona raisi?”

“Bado?”

Nikatoka katika chumba hichi. Nikawaon amagaidi wawili wakikatiza moja ya kona katika kordo hii. Nikaanza kuwafwata kwa nyuma kwa mwendo wa kasi sana. Kitendo cha kuwakaribia, moja akageuka na kushangaa. Sikuhitaji kuwa na huruma wala maelezo mengi, nikawatandika risasi za haraka haraka na wakaanguka chini. Nikaendelea kuwau magaidi hawa kimya kimya ndani ya ndege hii pasipo wao wenyewe kugundua kinacho endelea. Nikasimama kwenye chumba ambacho nje walikwua wamesimama magaidi wawili ambao tayari nimesha waangamiza. Alama katika simu yangu ina onyesha kwamba eneo hili ndipo raisi alipo. Nikafungua mlango wa chumba hichi taratibu, nikaingia kwa kasi ya ajabu huku nikiwa nina jibingirisha chini, magaidi watatu nilio wakuta ndani ya chumba hichi, wakabaki wakiwa wanaduwaa. Nikawatandika riasi magaidi hawa wote ambao wamewaweka chini ya ulinzi raisi, mke wake pamoja na wafanyakazi wengine kumi na mbili. Nikasimama taratibu huku nikiwa siamini kama nime mpata raisi akiwa hai.

“Nime mpata muheshimiwa raisi”

Nilizungumza huku nikimtazama raisi aliye fungwa kamba miguuni na mikononi huku akiwa amefungwa bandeji mdomoni mwake na uso wake umejaa damu na dhairi ana onyesha amepigwa kipigo kikali. Nikasikia shangwe ikulu kwa mana katika kofia yangu niliyo ivaa ina kamera inayo rekodi matukio yanayo endelea eneo hili. Nikamfungua raisi kamba hizi.

“Muheshimiwa unajisikiaje?”

“Ninasijisikia vizuri X.”

Raisi alizungumza huku akitabasamu. Nikamkabidhi bastola yangu moja huku nikiendelea kuwafungua wafanyakazi hawa wa raisi, wakiwemo washauri wake, wapishi na kadhalika.

“Judy na Mau muna dakika mbili za kuja katika ndege hii. Siwezi kutoka na kupambana na watu wengine”

“Tupo njiani X”

Nilisikia Judy akizungumza. Nikatoka ndani ya chumba hichi na nikaufunga mlango wa ndege hii ili maadui ambao wapo nje wasiweze kuingia ndani ya ndege hii.

“Marubani wapo wapi?”

“Rubani mkuu ameuwawa na msaidizi wake ndio msaliti na amejumuika na magaidi hawa”

“So nani ata iendesha hii ndege?”

Nilimuuliza raisi huku nikimtazama kwa mshangao. Judy na Maulid wakafanikiwa kuingia ndani ya ndege kwa mlango wa siri nilio pitia mimi.

“Kuna anaye weza kuendesha ndege hii?”

Niliwauliza wafanyakazi hawa na hapakuwa na hata mmoja ambaye aliweza kunijibu. Nikaingia katika chumba cha marubani.

“Jamani hatuna rubani nina omba msaada”

“Mimi nina idea kidogo”

Judy alizungumza huku akikaa kiti cha pembeni yangu. Raisi naye akaingia ndani ya chumba hichi.

“X”

“Ndio mkuu”

“Ninashukuru sana kwa kuja”

“Usijali muheshimiwa, kwa sasa ina bidi tuondoke hapa”

“Ndege yangu haiingizi risasi wala bomu hivyo tupo salama”

“Sawa muheshimiwa, ila ishu ni jinsi gani tuna iendesha”

“X una nisikia”

Niliisikia sauti ya makamu wa raisi.

“Ndio”

“Kuna rubani hapa ata waelekeza.”

“Okay, Judy si una sikia vizuri?”

Nilimuuliza Judy ambaye amekaa kulia kwangu

“Ndio”

Tukaanza kupewa maelekezo mambo ya kufany hii ikiwa ndio mara yangu ya kwanza kuendesha ndege. Jambo la kumshukuru Mungu, Judy ana tambua baadhi ya mambo.

“Zungusha hicho kifaa kilicho andikwa eng start, kisha pandisha juu eng namba 1, 2, 4 na 4”

Judy aliniambia na mara baada ya kuminya baadhi ya batani. Taratibu ndege ikaanza kuwaka jambo lililo wastua magaidi hawa katika kambi yao hii. Wakaanza kushambulia kwa risasi ila hazikuweza kupenya kwenye ndege hii iliyo tengenezwa kwa ubora wa hali ya juu wa kumlinda raisi wa Tanzania.

“Mkuu ina bidi tuigeuze”

Judy alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.

“Sasa na hivi vibanda ina kuwaje?”

“Hakuna jinsi ni lazima iwe hivyo kwa maana run way ipo nyuma yetu”

“Ohoo Mungu tuokoe sasa mbona hii ndege haina mskani?”

Nilizungumza huku nikimtazama Judy usoni mwake. Akatabasamu, huku akionyesha kwa kidole.

“Hicho kirungu kushoto kwako ndio kina control kila kitu”

Nikakishika kifaa hichi na taratibu na kwa umakini mkubwa sana nikaanza kuizungusha kushoto kwangu ndege hii.

“Una weza kutazama camera system hapo ukajua namna ya kuvikwepa hivi vibanda”

Judy alizungumza huku akinionyesha kwenye tv ndogo iliyopo pembeni yangu upande wa kulia jinsi kemera ya juu na kamara ya mbele inayo onyesha eneo la nje la ndege hii.

“Ohooo……”

Nilizungumza huku nikiendelea kuigeza ndege hii na jambo la kumshukuru Mungu nikafanikiwa. Nikaanza kusukuma mbele taratibu gia iliyo mkono wangu wa kulia, huku jasho likinimwagika uso mzima kwa maana maadui wana zidi kutushambulia na mbaya ni kwamba barabara hii ya kuendeshea ndege ni ya vumbi hivyo kuna muda matairi ya ndege yana ingia kwenye mashimo mashimo. Ndege ikazidi kukolea kasi huku nikiyasikilizia jinsi mapigo ya moyo yanavyo kwenda spidi.

“Ongeza spidii mbele run way ina isha mkuu”

Judy alizungumza huku macho yakimtoka kwa maana zimebaki mita chache sana barabara hii kufika mwisho. Misuli ya mkono wangu wa kulia ikazidi kutuna taratibu ndege ikaanza kunyanyuka mbele taratibu na baada ya muda kidogo ikaacha ardhi na kupaa angani huku nikiipunyua punyua miti ya msitu huu na matairi ya nyuma. Nikashushua pumzi nyingi sana mara baada ya ndege hii kukaa sawa angani na nikasikia shangwe kutokea ikulu watu wakifurahia sana kwani nime weza kumuokoa raisi pamoja na ndege yenta thamani ya dola za kimarekani milioni mia tano. Nikaigeuza taratibu na ikakaa usawa wa kuelekea Tanzania, kisha Judy akaniambia niminye batani iliyo andikwa auto pilot.

“Kazi nzuri mkuu, sasa ndege ina jiendesha yenyewe”

“Kweli?”

“Hali ya Mungu vile”

“Hongera sana X”

Makamu wa raisi alizungumza.

“Nashukuru mkuu. Naweza kuzungumza na mke wangu”

“Ndio”

“Tafadhali naomba niongee naye”

“Dakika tano”

Nikafungua mkanda wa siti hii ya rubani na sasa kidogo amani ikataala moyoni mwangu.

“Mke wako una weza kuzungumza naye sasa”

“Holoo”

Niliisikia sauti ya Cauther.

“Yes baby, nimefanikiwa”

“Kweli?”

“Haki ya Mungu vile nime fanikiwa now nipo njiani nina rudi nchini Tanzania”

“Hongera sana mume wangu”

“Nina shukuru. Baada ya masaa kadha nita kuwa nchini Tanzania”

“Nakusubiria kwa hamu mume wangu”

“Niombee”

“Toka ulipo ondoka mume wangu nilikuwa nina kuombea”

“Nashukuru”

“Sinto lala hadi ufike”

“Sawa mke wangu”

Nikamaliza kuzungumza na mke wangu kisha nikanyanyuka kwenye siti hii.

“Yaliyo baki si una weza kumalizia?”

“Ndio”

Judy alinijibu huku akiwa amejawa na tabasamu usoni mwake. Nikamtazama kwa sekunde kadha kisha nika mpa tano kwa mkono wangu wa kulia. Tukagonganisha ngumi zetu kisha nikatoka ndani huu.

“Muheshimiwa raisi yupo wapi?”

“Chumbani kwake pamoja na mke wake”

“Ume fanya chake up ya ndege nzima na kudhibitisha hakuna adui aliye baki?”

“Yaa nimekagua kila eneo”

“Mauiti za maadui zipo ngapi?”

“Kumi na mbili”

“Maiti za watu wetu”

“Kumi na nane”

“Duu ni pigo”

Nikaachana na kusimama mlangoni mwa chumba cha raisi. Nikagonga na akafungua mlango.

“Karibu sana X”

“Nina shukuru”

Nikaingia ndani ya chumba hichi na kumkuta mke wa raisi akiwa amekaa kwenye sofa huku akionekana kuwa katika hali ya butwaa.

“Madame yupo salama?”

“Ndio hajaweza pata majera ila amewapoteza walinzi wake wanne na hili tukio kidogo limeweza kumfanya awe katika wakati kama huu”

“Pole”

“Nashukuru na hongera sana kwa kazi nzuri X. Hakika sinto sahau hili ulilo lifanya na pia nina omba tukifika salama nchini Tanzania, tafadhali rudi kazini, nchi ina kuhitaji, watu wana kuhitaji. Tafafhali unda kikundi kingine cha X ambacho kitakuwa kina saidia taifa kwenye kipindi kama hichi, nipo chini ya miguu yako”

Raisi alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake. Nikastuka sana mara baada ya kumuona akipiga magoti chini kuniomba jambo lililo nifanya nimnyanyue haraka kwa maana mtu mwenye heshima kubwa kama raisi hapaswi kinipigia magoti hata siku moja kwa maana mimi nipo chini yake.



“Muheshimiwa pasipo kukuvunjia heshima. Samahani sana hii ndio ilikuwa ni kazi yangu ya mwisho kabisa kuifanya katika serikali yako. Ninaomba niweze kukurudisha Tanzania salama kisha baada ya hapo nita endelea na maisha mengine kwa maana ni jana tu nimetoka kufunga ndoa hivyo hata maisha ya ndoa bado sija yafaidi”

Raisi akanitazama usoni mwangu huku akiwa amejawa na uso wa huzuni. Nikamtazama mke wake kwa sekunde kadha kisha nikatoka ndani hapa. Nikarudi katika chumba cha marubani na tukaendelea na safari. Tulivyo kabiria kuingia katika anga la Tanzania ndege nne za kivita aina ya Jet zikatusindikiza ili kuimarisha ulinzi zaidi.

Tukafanikiwa kufika katika kiwanja cha mwalimu J. K Nyerere majira ya saa nane usiku. Kutokana na maelekezo tunayo endelea kupatiwa na warubani walipo ikulu, tukafanikiwa kuitulisha ndege hii salama Salmin huku furaha zikiwa zime tawala kwa kila mtu. “

“Dogo hongera sana”

Nilizungumza huku nikimtazama Judy usoni mwake.

“Nashukuru mkuu”

Nikafungua mkanda wa siti yangu na kusimama.

“Mkuu”

“Ndio”

“Nashukuru kwa kutuokoa mimi na Maulid”

“Musijali, next time ina wapasa muwe makini sana”

“Sawa mkuu”

Nikatoka katika chumba hichi na kukutana na Maulid. Akanipigia saluti ya heshima.

“Hongera sana mkuu”

“Nashukuru, muheshimiwa raisi na mke wake wana hali gani?”

“Wapo salama mkuu”

Muheshimiwa raisi na mkewe wakatoka katika chumba chao. Nikampigia raisi saluti huku nikimtazama usoni mwake.

“Karibu tena nchini mwako muheshimiwa”

“Nina shukuru sana X”

Mlango wa ndege ukafunguliwa na taratibu tukaanza kushuka kwenye ngazi hizi ndege kuelekea chini. Raisi akapokelewa na makamu wa raisi aliye ongozana na walinzi lukuki kuhakikisha kwamba usalama wake una zidi kuimarishwa.

“X”

Makamu wa raisi aliniita huku akinisogelea.

“Ndio muheshimiwa”

“Hongera sana na nina shukuru”

“Usijali mkuu”

“Nime kuja na mke wako yupo kwenye gari”

“Gari gani?”

“Lile pale”

Makamu wa raisi akanionyesha gari ambao yupo mke wangu. Nikatembea kwa haraka hadi katika gari hilo. Mke wangu akashuka kwa haraka na akanikumbatia kwa nguvu zote. Tukanyonyana denda kwa furaha sana.

“Nimerudi mke wangu”

“Hongera sana baby”

“Nina shukuru”

“Makamu wa raisi ametuzawadia hili gari kama zawadi ya arusi”

“Waoooo”

Nilizungumza huku nikiitazama hii gari aina ya BMW X5.

“Amenikabidhi funguo pamoja na kazi za gari”

“Amekukabidhi muda gani?”

“Majira yale ya saa nne hivi usiku”

Nikamtazama makamu wa raisi, ambaye naye kwa bahati nzuri ana nitazama. Akanikonyeza huku akininyooshea kidole ngumba, akanipa ishara kwamba ata nipigia simu. Akaingia kwenye gari lake na wakaondoka uwanjani hapa na msafara wa walinzi wake pamoja na walinzi wa raisi.

“Mkuu”

Maulid na Judy wakanifwata sehemu nilipo simama na mke wangu.

“Niambieni wadogo zangu”

“Tuna tamani kwa kipindi kingine tuweze kufanya kazi kwa pamoja”

“Hahaaa…tuombe uzima. Alafu sijawatambulisha kwa mke wangu. Mke wangu huyu ana itwa Judy na huyu ni Maulid nilikuwa nao katika kazi hii ya kumuoka raisi”

“Nina shukuru kuwafahamu jamani”

“Hata wewe tuna shukuru kukufahamu”

“Mkuu, wifi yangu ni mzuri saa. Umejua kuchagua”

“Hahaa nina washukuru. Muna rudi kambini?”

“Ndio”

“Kuna hizi nguo na silaha nahitaji murudi nazo kwa maana mimi nina endelea kula honeymoon yangu na mke wangu”

“Hahaa sawa mkuu”

“Mume wangu ndani ya gari hakuna nguo. Labda uwakabidhi silaha tu”

“Sihitaji haya mavazi yanizoee. Una jua madhara ya kuendelea kuwa nayo mwilini?”

“Mmm”

“Ni kujikuta una yapenda na nina rudi kazini ikiwa sihitaji kurudi kazi”

“Sawa, sasa uta vaa nguo gani mume wangu”

“Una onaje mkuu tukapitia kambini pamoja kisha ukavaa nguo zako na ukaenda na wifi hotelini”

“Hapo ume nena Judy”

Tukaingia kwenye gari hili wote wanne na tukaianza safari ya kuelekea katika kambi ya jeshi la anga. Tukafika kambini, mimi, Judy na Maulid tukashuka kwenye gari. Nikakabidhi silaha nilizo zichukua katika ghala la silaha. Nikabadilisha mavazi yangu, nikaagana na Maulid, Judy pamoja na mkuu wa kambia kishi nikarudi ndani ya gari na kuianza safari ya kuelekea hotelini.

“Kweli mume wangu nime amini kwamba wewe ni X”

“Kwa nini ume amini sasa hivi?”

“Una jua nilipo kuwa nime kaa pale ikuku, nikawa nina sikia sifa zako kwamba kama ume kabidhiwa hiyo kazi ya kumuokoa raisi basi ni lazima kazi ita kwenda vizuri na kwa haraka sana na kweli imekwenda kwa haraka”

“Kina nani hao walikuwa wana zungumza?”

“Vile vidada ulivyo niacha navyo. Vilitokea kunizoea balaa yaani wana nimwagia sifa kede kede kwamba nime bahatika kumpata mwanaume mzuri sijui nini na nini, yaani maneno yalikuwa mengi sana”

“Yaani nika hisi kwamba wana kutaka”

“Achana nao”

Tukafika hotelini, tukaoga kwa pamoja na mke wangu. Kutokana na uchovu wa kazi ngumu iliyo kuwa mbele yangu, ikanibidi nilale pasipo kufanya chochote na mke wangu..

Mlio wa simu ya mke wangu ukanifanya nifumbue macho yangu yaliyo jaa uchovu wa usingizi. Nikatazama pembeni na kumuona mke wangu akiwa wamelala fofofo. Taratibu nikaichukua simu hiyo na kutazama ni nani ambaye ana piga. Nikakuta ni namba ya mama mkwe, nikatazama saa ya simu ina onyesha ni saa kumi na mbili na dakika kumi na tano. Nikataka kuikata simu hiyo ila nikajifikiria kwa sekunde kadhaa kisha nika muamsha mke wangu.

“Mmmm”

“Mama ana piga”

“Asubuhi yote hii”

Cauther alizungumza kwa sauti ya upole iliyo jaa uchovu mwingi sana. Akaipokea simu hiyo na kuiweka sikioni mwake.

“Shikamoo mama”

“What….?”

Cauther alihamaki huku akijigeuza na kukaa kitako kitandani jambo lililo nifanya na mimi kumtazama.

“Saa ngapi?”

“Nakuja mama”

Mke wangu alizungumza huku macho yakianza kububujikwa na machozi, ikiwa ni ishara kwamba kuna tatizo lime tokea kwao.

“Mume wangu baba ameshambuliwa na majambazi asubuhi hii amepigwa risasi amekimbizwa Muhimbili na hali yake sio nzuri kabisa mume wangu. Twende sasa hivi baby”

Mke wangu alizungumza huku akilia kama mtoto mdogo. Tukashuka kitandania, hapakuwa na hata aliye kumbuka kuoga. Tukavaa nguo zetu haraka haraka, tukaianza safari ya kuelekea Muhimbili. Tukafika Muhimbili saa moja na dakika tano, Cauther akampigia mama yake na kumuuliza ni wodi gani ambayo ame lazwa baba yake na akaelekezwa. Tukafika katika wodi hiyo na kukutana na kundi kubwa la ndugu wa Cauther ambao wote ni waarabu. Kaka yake akanifwata huku uso wake ukiwa umejawa na hasira kali sana.

“Ume fwata nini hapa wewe masikini”

“Kaka mbona una kuwa hivyo”

Cauther alizugumza huku akimshika mkono kaka yake.

“Niachie. Nakuuliza wewe masikini ume fwata nini hapa. Toka uwe na mdogo wangu ni mikosi tu kwenye familia yatu”

Shemeji yangu huyu alinishika shati langu eneo la kifuani mwangu na kunikwida kisawa sawa.

“Ondoka hapa wewe mbwa mweusi”

Shangazi yake Cauther alizungumza maneno makali sanaa ambayo hakika moja kwa moja yakapenya katika moyo wangu na kuniumiza sana.

“Nimesema muacheni mume wangu. Huyu ni mume wangu nimemchagua mimi sitaki munyanyaseee”

Cauther alifoka, manenes wawili wakatika katika chumba kilichopo eneo hili.

“Jamani tupo hospitalini na mgongwa ana shuhikiwa, hatuhitaji kelele kama kuna mambo yenu ya kifamilia katatueni nje ya hospitali hii”

Nesi mmoja alizungumza kwa ukali na kuwafanya waarabu hawa wanao nicharukia kutuliza mzuka kidogo.

“Vipi hali ya mgonjwa?”

Mama mkwe aliuliza huku akiwa an alia kwa uchungu sana.

“Bado tuna mshulikia, kelele zetu zita tufanya tushindwe kumuhudumia mgonjwa”

“Sawa wamenyamaza”

Mama mkwe alizungumza kwa ustarabu kisha manesi hao wakaorudi ndani.

“Oya nikifumba na kufumbua ondoka hili eneo halikuhusu”

Shemeji yangu alizungumza kwa sauti ya chini ila ya kunikoromea huku akiwa amenitunishia kifua chake. Nikamtazama Cauther ambaye kwa namna moja ana tamani kuondoka na mimi na namna nyingine ana hitaji kuaa hapa ili kufahamu hali ya baba yake ina endeleaje.

“Tuta wasiliana baadae mke wangu”

“Msamehe tu kaka yangu”

“Usijali nina elewa mke wangu”

Nikataka mbusu Cauther mdomoni mwake ila kaka yake akaingilia katikati, kitendo kilicho nifanya nikereke sana. Nikamshika kiganda chake cha mkono wa kulia na nikakiminya kwa nguvu huku nikimvuta karibu yangu na kumnong’oneza sikioni mwake.

“Nimesha muoa mdogo wako na ni mke wangu halali wa ndoa sasa. Ole wako siku nyingine ujaribu kunitunishia misuli yako ya kipumbavu nitakuvunja mbavu zako. Kenge wewe”

Nikamuachia kiganja chake kilicho jawa na uwekundu wa kuvilia damu kwa manaa nime mbana kisawa sawa. Nikaondoka eneo hili na kurudi ndani ya gari. Nikatoa simu yangu mfukoni na kumtext mke wangu.

‘Muulize mama ni eneo gani ambalo baba alishambuliwa na majambazi?’

Nikasubiria kama dakika mbili hivi, meseji kutoka kwa mke wangu ikaingia kwenye simu yangu.

‘Anasema kwamba ni dukani kwake kule Posta. Alikuwa ndio ana fungua, majambazi wakavamia na kuiba vito vyote vya dhahabu’

‘Sawa nita lishuhulikia ila usimuambie mtu’

‘Sawa mume wangu, nisaidie kuwakamata majambazi walio mdhuru mume wangu’

‘Usijali, baadae ukinihitaji niambie’

‘Sawa mume wangu’

Nikaondoka hospitalini na moja kwa moja nika elekea hadi eneo la Posta lilipo duka kubwa la baba Cauther linalo husika na uuzaji wa cheni, saa, mikufu pete vya dhababu. Kiufupi ni Sonara mkubwa sana anaye julikana katika jiji hili la Dar es Salaam. Nikakuta polisi wakiwa eneo hili, huku wakiwa wamezungushia utepe wa njano unao wazuia watu kuingia.

“Habari yako afande”

“Salama”

“Ahaa kume tokea nini hapa?”

“Asubuhi ya leo kuna majambazi wame vamia dukani hapa na wamempiga risasi mmiliki wa duka hili na kuiba mali zilizomo ndani hapa”

“Sawa sawa, nina weza kuingia ndani?”

“Hapana haturuhusu raisi yoyote kuingia”

Kutokana sina kitambulisho wala kitu chochote kinacho husiana na ufanyakazi katika kitengo chochote cha usalama, nikawa sina jinsi wala namna zaidi ya kurudi eneo nilipo simamisha gari langu. Nikajifikiria kwa sekunde kadhaa huku nikitazama jinsi waandishi wa habari wakipiga piga picha katika eneo hili.

“Oya mambo vipi kaka?”

Nilimuongelesha mmoja wa wandesha bodaboda aliye simama pembeni ya barabara.

“Salama niambie”

“Poa aisee ume weza kushuhudia kilicho tokea eneo hili?”

“Yaa asubuhi, kuna gari moja Brevis nyeusi ilisimama eneo lile pale pembeni ya duka. Wakashuka watu watatu wenye bunduki. Wawili wakaingia ndani na mmoja akabaki nje, wakaingia ndani ya duka hilo baada ya dakika tano wakatoka ila ndani tulisikia milio kama miwili ya risasi, kisha wakapotelea kwenye barabara ile”

“Ahaa sawa,muliweza kuona namba za gari hilo?”

“Yaa”

“Nitajie”

Jamaa huyu akanitajia namba za gari hilo, nikamshukuru kisha nikaondoka eneo hili kwa maana nimesha pata kwa kuanzia. Nikaitafuta namba ya Wille kijana ambaye kazi yake ni hacker(mdukuzi) ambaye kazi zake ana zifanya kwa siri sana n anime mfahami miaka minne sasa na nimekuwa nikimfichia siri ya kazi yake hiyo kwa maana kwa kupitia kazi yake hiyo ndio ina mfanya ana ishi mjini kwani ana uwezo wa kufunguo simu zote duniani ambazo zime fungwa, hata kama ni iphone ambazo husifika ni simu zenye ulinzi mzuri kuliko simu nyingine pale zinapo ibiwa.

“Dogo”

“Niambie kaka Eddy”

“Safi upo wapi?”

“Ahaa nipo home vipi kwema?”

“Sio kwema nahitaji kuonana na wewe muda huu”

“Ahaa kikawaida au kikazi?”

“Kikazi”

“Kuna tatizo?”

“Sio lako ni tatizo langu”

“Sawa kaka”

Nikakata simu, na kuelekea Mburahati, nikasimamisha gari mbele ya moja ya duka la Masawe, jamaa ninaye juana naye vizuri.

“Aiisee chalii yangu hiyo BM 5 ime itolea wapi?”

“Hahaa ipo dukani hiyo chalii yangu”

“Aisee ila imekufaa mwanangu fanya uichukue wewe mwenyewe”

“Ahaa wapi mwanangu, hela nazitoa wapi usawa wenyewe ziro ziro. Aisee naingia huko kati hembu nichekie hii ndinga”

“Usijali chalii yangu”

Nikaanza kukatiza katika vichochoro vya nyumba zilizo jengwa pasipo mpangilio maalumu. Nikafika katika nyumba anayo ishi Willey eye mwenyewe. Akanikaribisha ndani.

“Kumebadilika mdogo wangu, naona una ma computer mapya”

“Yaa teknolojia ime panda hivyo na mimi nime badilika”

“Aisee nahitaji unitafutie namba za hili gari. Nahitaji kujua lipo wapi kwa maana leo asubuhi hii lime fanya uhalifu eneo la Posta so nahitaji kufahami ni mali ya nani”

“Sawa kaka”

Nikamtajia Wille namba hizo na akaanza kazi ya kutafuta gari hilo lilipo.

“Hizi ni video nilizo zipata kwenye kamera za cctv za pale posta. Baada ya hapo likaondoka na kuelekea maeneo ya Bagamoyo.”

“Una weza kuzipata sura za hao mahambazi?”

“Ngoja mara moja”

Wille akaanza kuzi scan picha za majambazi hao watatu na akafanikiwa kuzipata sura zao. Wote ni waarabu, tukayapata majina yao.

“Una weza kugundua kwamba watu wao wa karibu ni nani?”

“Ngoja nizi tafuta picha zao Instergram”

Vidole vya Wille au William vikazidi kuongeza kasi katika kutafuta picha za watu hao watatu. Tukabaki tukiwa tumejawa na mshangao mara baada ya kuziona picha kadhaa za majambazi hawa wakiwa wamepiga picha na shameji yangu kaka yake Cauther ambaye masaa machache yaliyo pita ametoka kunikoromoea hospitalini.



“Huyu si shemeji yako?”

“Ndio”

“Ina maana ana wafahamu hawa watu?”

“Ndio hapa ina bidi tufahamu hili”

“Ila kaka hii familia si haikupendi kabisa, sasa una wasaidia kwa nini?”

“Nina fanya kwa ajili ya mke wangu sio kwa ajili yao”

“Sawa kwa maana ingekuwa sikujui labda ninge kushauri jambo jengine ila kutokana nina kujua na nina jua uwezo wako na wewe ni nani basi nita kusaidia ndugu yangu”

“Nashukuru alafu kuna siku nita kuhitaji ufanye kazi na serikali. Haya maish aya kujificha ficha huku na kupata pesa za kuunga unga sio nzuri ndugu yangu”

“Ila serikali ita kubali watu wa aina yetu?”

“Yaa tena nyinyi ni watu muhimu, ukitazama nchi yetu ina ongoza kwa uchumi mkubwa sasa Afrika na teknolojia imekuwa kubwa sana, so wait for my call”

“Nashukuru sana kaka”

“Niingizie hizi video, picha kwenye simu yangu”

“Sawa”

Baada ya Willy kukamilisha kazi hiyo nikampatia kiasi cha shilingi elfu hamsini kisha nikaondoka nyumbanii kwake. Nikapita kwa mangi, nikaagana naye na nikaondoka eneo hili na kuelekea hospitali ya Muhimbili. Nikafika katika maegesho ya magari, nikampigia simu Cauther na akanifwata sehemu nilipo.

“Vipi hali ya baba?”

Nilimuliiza mke wangu mara baada ya kuingia ndani ya gari.

“Bado hawajamtoa chumba cha upasuaji”

“Duu oparesheni yake ime chukua muda mrefu”

“Yaa yaani hadi nime poteza amani mume wangu”

“Vipi askari wana semaje?”

“Hata sijui kwa maana kaka ndio alikuwa ana zungumza nao”

“Okay. Sasa mke wangu nime weza kulifwatilia hili swala ka umakini wa hali ya ajuu”

“Ehee ume gunduaje?”

“Kuna hizi video”

Nikaanza kumuonyesha video ya kwanza mke wangua mbayo ina waonyesha majambazi hao watatu jinsi wanavyo shuka kwenye gari na kuingia ndani ya duka la baba yake, wakafanya tukio kisha wakatoka na kuondoka kwa kasi.

“Hii gari mmiliki wake bado hatujampata kwa maana hizi plate namba ni feki. Pia tume weza kutambua kwamba hawa majambazi ni watu kutoka Oman. Hembu watazame sura zao una zifahamu?”

Mke wangu akatazama picha hizo kisha akatingisha kichwa akimaanisha kwamba hawajui kabisa.

“Upelelezi haukuishia hapo, tukagundua kwamba hawa majambazi ni rafiki wa kaka zako na hizi picha tume zikuta kwenye instergram page yake”

Mke wangu macho yakamtoka huku akiweka mkono mmoja mdomoni.

“Kwa hiyo Salum ana wafahamu?”

“Hadi kupiga nao picha ina maana ana wajua na sio picha moja ni picha kama sita hivi na katika nyakati tofauti tofauti”

“Ngoja nimpigie simu mshenzi, ana wakaribisha majambazi kwenye familia alafu ana taka tumchekee tu”

“No usimpigie”

“Kwa nini mume wagu ikiwa majambazi ndio hao hapo?”

“Ndio nina hitaji kulichunguza hili jambo kwa umakini sana. Kwa ni sasa hivi yupo wapi kaka yako?”

“Alitoka na askari na sifahamu amekwenda wapi kwa maana hakumuaga mtu yoyote yule”

“Nipatie namba ya kaka yako”

“Sawa”

Cauther akanitajia namba ya kaka yake anaye itwa Salum. Nikainakili kwenye simu yangu.

“So hotelini leo kuna rudikika au nifanye mpango wa kurudi kulala nyumbani?”

“Hata sielewi mume wangu, ngoja tuone hali ya baba ita kuwaje kisha nita kuambia”

“Sawa mke wagu, ila hili jambo usimueleze mtu yoyote hadi pale nitakapo maliza uchunguzi wangu”

“Sawa mume wangu. Nina kupenda sana”

“Nina kupenda pia mke wangu”

Nikamnyonya denda mke wangu kwa dakika kadha kisha akashuka ndani ya gari na kuelekea alipo iacha familia yake. Nikajifikiria kwa dakika kadhaa kisha nikaitafuta namba ya makamu wa raisi na nikampigia simu.

“Ndio X”

“Heshima yako”

“Nashukuru sana”

“Mzee wangu nina shida moja”

“Shida gani?”

“Kuna hili tukio la ujambazi lililo tokea asubuhi ya leo hapo Posta”

“Ndio ndio nililisikia?”

“Aliye shambuliwa na kupigwa risasi ni baba yangu mkwe. Hivyo nina hitaji kufanya upelelezi wa hili tukio, ila sio kwamba nina rudi kazini ila nina fanya personal”

“Nakuelewa X, ila tambua kwamba huna mamlaka yoyote ya kufanya chochote kihusianocho na usalama?”

“Nalitambua ndio maana nime kupigia kukuomba msaada na sio msaada wa kulimamka zaidi bali nina hitaji pia wale vijana wawili nilio fanya nao kazi jana wanisaidie katika hili”

“Mmmmm sawa. Uta chukua muda gani?”

“Siku moja ina nitosha”

“Sawa, nina wapigia simu na kuwapa namba yako. Wata kupigia na uta jua ni wapi ulipo basi muta shirikiana. Wezako wana vitambulisho, je uta hitaji kitambulisho cha dharura?”

“Hapana muheshimiwa. Vitambulisho vyao vina tosha kabisa”

“Je umeweza kutambua ni kina nani kwa maana hadi sasa sijasikia ripoti yoyote kutoka kwa askari na sidhani kama wana weza kuwatambua?”

“Siku nyingi sana nimesha weza kuwajua. Ila ripoti kamili nitakuletea mara baada ya kazi kuisha”

“Nina kupenda hapo tu X mambo yako una yapeleka chap chap. Ukihitaji kurudi kazini basi milango ipo wazi”

“Nina kushukuru mzee wangu. Pia nina shukuru kwa hii BMW X5”

“Usijali na pesa ya kazi yako imesha ingizwa kwenye akaunti yako ile ya kazi toka asubuhi”

“Sawa nina shukuru mkuu”

“Nawe pia nina shukuru, raisi amenidokezea kwamba ata kualika chakula cha usiku ikulu wewe na wezako, ila sijajua ni lini kwa maana kwa sasa wana fanyiwa canceling kidogo kwani tukio lilikuwa ni la kinyama sana”

“Hakuna shaka mzee uta nifahamisha tu”

“Sawa”

Makamu wa raisi akakata simu na baada ya dakika mbili simu yangu ikaanza kuita na namba ngeni ndio inayo nipigia.

“Mkuu ghabari yako”

“Safi Judy upo wapi?”

“Nipo Masaki Mkuu”

“Ndipo unapo ishi?”

“Ndio ndio”

“Okay sasa fanya hivi nahitaji tuonane sasa hivi, mpitia Maulid nawahitaji kikazi ila ni private work”

“Sawa mkuu hakuna shaka”

“Poa hembu ngoja usikate nina poke simu”

Nikaisubirisha simu ya Judy kisha nikaipokea hii namba mpya inayo ingia kwenye simu yangu.

“Mkuu, Maulid hapa”

“Tena nilikuwa nina zungumza na Judy sasa hivi nina wahitaji kikazi muda huu”

“Sawa sawa mkuu hakuna shaka”

“Upo wapi?”

“Mikocheni”

“Jiandaeni na silaha zenu ila muvalia kiraia. Sawa”

“Sawa mkuu”

“Judy atakupitia muta nikuta maeneo ya Fire hapa”

“Sawa sawa mkuu”

“Harakisheni, muda tulio nao ni mdogo”

“Sawa”

Nikakata simu ya Maulid na nikaendelea kuzungumza na Judy.

“Sasa Judy nimezungumza na Maulid yupo Mikocheni, uta mpitia na muta nikuta hapa Fire”

“Sawa je tuje na magari yetu au?”

“Hapana gari lipo, munaweza kodisha bajaji kuepuka foleni”

“Sawa sawa”

Nikaakta simu, nikawasha gari na nikaondoka hapa Muhimbili, moja kwa moja nika elekea hadi eneo la Fire. Nikaa kwa muda wa dakika arobaini na mbili hivi, nikawaona Maulid na Judy wakishuka kwenye moja ya bajaji. Kutokana wana lifahamu gari langu, hawakuwa na haja ya kunipigia simu. Wakatembea hadi eneo nilipo, Judy akaingia siti ya mbele na Maulid akapanda siti ya nyuma. Nikasalimiana nao kwa kupeana nao tano.

“Aisee madogo kumbe mukiwa kitaa muna kuwa mabishoo ehee?”

“Kiasi chake mkuu”

“Naona Judy ume kuwa bonge la sister duu. Sasa mapigo ya mavazi hayo ndio ninayo yahitaji kwa maana hawa Kenge ninao wafwatilia ina onyesha ni watu wana penda sana kula bata.”

Nikaanza kuwaeleza tukio zima zilivyo kuwa na nikawaonyesha video pamoja na picha za majambazi.

“Hapa mkuu ina bidi tuanze kumfwatilia huyu Salumu shemeji yako?”

Maulid alishauri huku akitazama picha za Salumu pamoja na majambazi hao.

“Yaa ndio maana maana nikawahitaji. Nahiataji tumteke huyu Salumu, tukisha mteka basi tuta anza kumuhoji maswali”

“Mbona kumteka tuna kuwa tuna kwenda mbali mkuu. Huyu tuna mbananisha sisi kama sisi”

Judy alishauri.

“Hapana, katika familia yao hawanijui mimi ni nani na wote wana nijua mimi ni kama dereva taksi na mtu wa kawaida sana.”

“Hilo tutalifanya sisi mkuu wewe wala hauto kuwa na haja ya kuhangaika”

“Sawa nime walewa na nina waamini. Hii kazi japo ni ndogo ila ina hitaji umakini kwa maana tuna hitaji kufahamu mzunguko mzima una kuwa vipi”

“Hakuna shaka mkuu”

Nikampigia simu Wille.

“Kaka”

“Naam sasa nina kutumia namba ua Salumu, nahitaji kufahamu phone record zake zote za wiki hii, pia nina hitaji kujua ni wapi alipo”

“Sawa kaka ila nilisha mtracke na gari lake. Sasa hivi anaelekea Mbezi ya Kimara”

“Okay nitumie ramani yake kwenye simu yangu”

“Sawa”

Nikakata simu na nikawasha gari na kuanza kuondoka eneo hili kwa mwendo wa kasi ili kuhakikisha kwamba tuna mpata Salumu. Jambo la kumshukuru Mungu ni kwamba mchana huu hakuna foleni kubwa. Willey akanitumia gprs track inayo muonyesha ni wapi Salumu ana elekea. Nikaipokea simu ya Willey.

“Kaka umeipata?”

“Ndio nina ona ana elekea njia ya Goba. Nisaidie jambo moja”

“Ndio”

“Cheza na taa zote za barabarani. Nahitaji kijani”

“Nimekusoma kaka na nina kuona”

Nikazidi kuongeza mwendo kasi wa gari hili ambalo ni jipya kabisa. Ili niwahi zaidi nikatumia njia ya mabasi ya mwendo kasi. Eneo la Ubungo mataa nikapita kama mshale hadi Judy na Maulid wakashangaa.

“Mkuu upo spidi”

Judy alizungumza huku akitupia jicho kwenye dashboard na kuona mshale wa spidi ukielekea kwenye miambili.

“Yaa huyu mjinga ina bidi tumpate tu.”

Jambo la kumshukuru Mungu ni kwamba barabara sasa ni pana kuanzia kimara mwisho hadi mbeni. Ndani ya dakika kumi nikafika Mbezi mwisho na kuingia upande wa kulia kwangu na kuishika barabara ya goba.

“Yupo kwenye barabara ya kuelekea Madale”

Judy alizungumza huku akitazama gprs track iliyopo kwenye simu yangu.

“Poa”

Kutokana na ujuzi wangu wa uendeshaji wa magari na kuzifahamu barabara za jiji hili la Dar es Salaam, haikuwa kazi ngumu kwa mimi kuweza kumfikia Salumu ambaye mwenyewe hajui kama nina mfukuzia. Tukamuona umbali wa mita thelathini kutoka sisi tulipo na katikati yetu tume tenganishwa na magari mawili.

Tukaendelea kumfwatilia Salum hadi kwenye moja ya jumba la kifahari. Akapiga honi getini na taratibu geti likafunguka na akaingia ndani na geti likafungwa.

“Hili jumba ni la nani?”

Niliuliza.

“Mmm hata mimi sifahamu”

Judy alijibu huku tukiwa tumesimama mbali kidogo kutoka lilipo jumba hili. Nikampigia simu mke wangu.

“Baby ngoja mara moja baba ndio wamemtoa chumba cha wagonjwa”

Mke wangu alizungumza kwa sauti ya kunong’oneza.

“Ohoo sawa ila samahani mke wangu. Salumu yupo hapo?”

“Hajarudi bado”

“Hivi muna ndugu aliye jenga haya maeneo ya Madale?”

“Salumu ana nyumba yake huko”

“Okay”

“Mbona ume uliza?”

“Nimeuliza tu”

“Basi sawa baadae nita kujulisha kuhusiana na hali ya baba”

“Sawa mke wangu”

Nikakata simu.

“Ana sema kwamba ni nyumba ana nyumba huku, nahisi ndio hiyo.”

So tuna fanyaje mkuu”

“Ngoja kwanza tumpe muda kidogo”

Tukasubiria kwa muda kidogo, wote tukastuka mara baada ya kuina gari ya majambazi iliyo fanya uhalifu Posta ikisimama nje ya geti hilo huku ikiwa ime fungwa namba nyingine kabisa tofauti na namba zilizo fanya tukio.

“Mmmm hii si ndio hii gari?”

Judy alizungumza huku akitazama kwenye video gari hiyo, ambayo taratibu imeanza kuingia ndani ya jumba hilo.

“Ndio hiyo hiyo. Wamepiga tukio alafu wamebadilisha namba”

“Tunafanyaje mkuu?”

Maulid alizungumza huku akinitazama. Nikakaa kimya huku nikitazama jumba hili kwa umakini sana, nikazihesabu kamera zote zilipo katika eneo hilo zinazo onekana kwa nje.

“Muna dakika saba nahitaji muwanyamazishe walipo ndani na baada ya hapo nahitaji kuzungumza na Salumu mimi mwenyewe”

“Sawa mkuu”

Maulid akafungua bagi lake la mgongoni akavaa gloves nyeusi na akamkabidhi Juduy gloves hizo. Wakavalia kofia nyuesi na kuzishusha kidogo usawa wa nyuso zao, Judy akanikabidhi bastola moja yenye magazine iliyo jaa risasi. Wakachomeka bastola hizo viunoni mwao kisha wakashuka kwenye gari.

“Musiue ila wanyamazisheni”

Nilizungumza huku nikiwa nimeshuha kioo cha upande wa Judy. Judy akaniyooshea dole gumba akimaanisha kwamba ame nielewa. Judy akatembea hadi katika geti na akaminya kitufe cha kengele, huku Maulid akiupanda ukuta huo kwa kasi ya ajabu sana hadi mimi mwenyewe nikashangaa.

‘Dogo yupo vizuri’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikisubiria matokea ya vijana wangu. Nikamuona Maulid akifungua geti hilo hapa damu ikaanza kunisisimka na nika jua tayari humo ndani kuna watu amesha watembezea kifinyo. Judy akaigia na baada ya dakika tano simu yangu ikaingia meseji kutoka kwa Judy akinipa taarifa kwamba niingie ndani.

‘Acha leo anijue mimi ni nani huyu kenge’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikishuka kwenye gari. Judy aliye simama gorofani akanipa ishara ya kuingia ndani. Kwanza eneo la nje, walinzi wawili wamelala chali wakiwa wamezimia, nikaingia sebleni na kupandisha gorofani, nikawakuta majambazi watatu wakiwa wamechakaa nyuso zao vibaya sana kwa damu, mikono yao na midomo yao ime fungwa na soltape kubwa.

“Shemeji shemeji niokoe hawa majambazi wamevamia nyumbani kwangu”

Kwa mara ya kwanza leo Salumu ana niita shemeji huku akiwa amepiga magoti chini huku mdomo wa bastola ya Maulid ukiwa umegusa kisogoni mwake na akifanya chochote basi anafumuliwa ubongo.



Nikampa ishara Maulid na akaitoa bastoka hiyo katika usogo wa Salumu. Nikaa kwenye moja ya sofa huku nikimtazama Salumu usoni mwake.

“Shemeji hawa ni kina nani?”

Nilimuuliza Salumu huku nikimtazama usoni mwake.

“Haha…ah…aha…awa ni rafiki zangu”

“Wana fanya kazi gani?”

“Ni wafanya biashara wa madini”

Salum alijibu huku akilia kama mtoto mdogo hadi nikamuonea huruma. Ubabe wote alio kuwa ana ufanya leo asubihi kwisha bahari.

“Una jua wamefanya nini?”

“Kivipi shemeji?”

“Baba yako si uja jua amevamiwa na majambazi?”

“Ndio na RPC ameniambia kwamba ata hakikisha kwamba ana wakamata majambazi”

“Umejuana nao kwa kipindi gani hawa?”

“Hawa?”

“Ndio hao?”

“Hawa nilikutana nao l ast year, nikawaunganisha na baba na wakafanya naye biashara”

“Okay kwa hiyo mahusiano yenu ni ya kibiashara?”

“Ndio”

Nikatoa simu yangu mfukoni na kumuonyesha video Salumu na rafiki zake hao wakifanya tukio katika duka la baba, mstuko alio upata Salumu, dhairi una onyesha kwamba hafahamu kama rafiki zake hao ni majambazi.

“Ku..kum….be hawa ndio walio mpiga risasi baba?”

“Ndio”

Salamu akasimama kwa hasira na akaanza kuwashambulia rafiki zake hao kwa ngumi na mateka. Ikanibidi kumuachanisha nao.

“Nitawaua wana haramu nyinyi. Kumbe mulikuwa muna nipaka mafuta kwa mgongo wa chuma. Haki ya Mungu baba yangu akifariki na nyinyi ni lazima niwaue”

Salumu alalama huku akiwa amejawa na hasira.

“Tuna ushahidi wa kutosha kuweza kuwakamata. Ina bidi tuwapekeke polisi sasa hivi”

Nilizungumza huku nikimtazama Salumu usoni mwake.

“Ngoja kwanza nimpigie RPC”

“Askari wakifika katika eneo hili ita kugarimu, uta kuwa na maswali mengi ya kujibu. Hivyo acha tuwapeleke polisi”

“Sawa nina shukuru sana shemeji yangu”

Judy na Maulid wakawatoa majambazi ndani hapa na kuwapeleka katika gari.

“Tuongozane kuelekea polisi”

“Sawa”

Tukatoka na shemeji, mimi na yeye tukapanda katia gari lake pamoja muhalifu mmoja huku waalifu wawili wakipanda katika gari langu. Ukimya ukatawala ndani ya gari hili la shemeji huku tukizidi kuwafwata Judy na wezake ambao wametutangulia.

“Shem”

Salumu aliniita.

“Naam”

“Umewafwatiliaje fwatiliaje hawa watu na kuwajua?”

“Hao jamaa wawili ni wana usalama, hivyo niliwaeleza juu ya tukio hili, wakanisaidia na tumefanikiwa kuwapata”

“Aisse nashukuru sana. Pia nisamehe kwa hapo awali kukuchukulia kama mtu mbaya. Sikufahamu kwamba moyo wako ni wa kujitoa hata kwenye matatizo yasiyo kuhusu”

“Usijali, nilizungumza na Cauther ameniambia kwamba baba amesha tolewa chumba cha upasuaji”

“Nita wasiliana nao baadae acha kwanza hawa washenzi wakashuhulikiwe”

Tukafika katika kiyuo kikuu cha polisi na nikawakabidhi waalifu hawa kwa askari ambao nao wakashangaa kukamatwa kwao. Nikawakabidhi na ushahidi wa video. RPC akanitiita pembeni kwa ajili ya kuzungumza naye

“Samahani kijana”

“Bila samahani”

“Una weza kuniambia ni mbinu gani ambazo ulitumia kuupata huu ushahidi?”

“Hapana siwezi kukuambia”

“Kwa nini?”

“Kikubwa ni kushukuru Mungu tume weza kuwasaidia kwa kiwango hicho tulicho wasaidia”

Nilizungumza kwa kujuamini huku nikimtazama RPC usoni mwake.

“Kijana wewe ni nani hadi una nijibu mimi hivyo. Afande Juma, hembu muwekeni ndani huyu mpuuzi”

“Ni wekwe ndani kwa kosa gani?”

“Lazima utuambie nani amekupatia huo ushahidi”

RPC alizungumza kwa kujiamini sana. Judy na Maulid mara baada ya kuona misukosuko ya kugoma kushikwa na askari hawa wawili wakashuka kwenye gari kwa haraka na kufika eneo la tukio. Baadhi ya askari kama sita hivi nao wakwa wamesha jiandaa kunihimili.

“Mkuu wana taka kufanya nini?”

Maulid aliuliza huku akiwatazama askari hawa usoni mwao.

“Mkuu tuwazingue?”

Judy alizungumza huku akiwatizama usoni mwao askari hawa.

“Nyinyi ni kina nani?”

RPC aliuliza huku akitukazia macho.

“Judy musitoe chochote. Sikiliza nilifanya kazi kwa ajili ya kumsaidia baba yangu mkwe tu. Hivyo basi sihitaji kugombana nanyi. Waambie vijana wako waniachie”

“Hamuna mamlaka ya kuzungumza chochote mbele yangu. Wakamateni wote muwaingize ndani”

RPC alizungumza kwa jeuri na kiburi, askari wake wawili wakanishia mmoja mkono wa kulia na mwengine mkono wa kushoto. Kitendo hicho kikawanyima uvumilivu Maulid na Judy, nikastukia askari hao wakianguka chini mara baada ya kukatwa mitama ya kustukiza na Maulid pamoja na Judy ambao wamejiandaa kwa lolote. Askari mmoja akanitandika ngumi ya kifua, jambo lililo nikasirisha sana. Nikamtandika teke lililo mrudisha nyuma kwa kasi ya ajabu na akaanguka chini. Nikamuona Salumu macho yakimtoka kwa mshangao, kwa maana hakutegemea kama tuta fanya jambo hili.. Askari hawa wakaanza kupambana nasi, sikuhitaji kuuficha uwezo wangu mbele ya Salumu. Ndani ya dakika kadhaa askari hawa wote tukawaadhibu vikali pasipo RPC wao ambaye ametoa maagizo ya kipumbavu. Maulid na Judy wakatoa vitambulisho vyao na kumuonyesha RPC, macho yakamtoka huku mwili ukimtetemeka.

“Hivi ndiovyo unavyo waongoza vijana wako?”

Nilimuliza RPC huku nikimtazama usoni mwake.

“Shukuru Mungu vijana wangu leo hawapo kwenye mood mbaya ila kama wangekuwa katika mood mbaya wangewaua vijana wako. Alafu jambo hili nita lifikisha kwa wakuu wako ikiwezekana upelekwe mbali na Dar es Salaam. Alafu askari gani una tumbo kubwa kama mama mjamzito. Hivi vita ikitokea sasa hivi uta weza kuruka vihunzi wewe?”

Nilizungumza kwa msisitizo huku nikiwa nimemsogelea RPC karibu kabisa na uso wake.

“Ahaa samahani mkuu nina omba yaishie hapa hapa”

“Nyinyi ndio wala rushwa wakubwa. Matumbo yame wafumuka kama……”

Nikataka kumtukana ila nikaishia kati.

“Shemeji tuondoke”

Nilimuambia shemeji huku nikimtazama usoni mwake. Salumu muda wote akawa kama mtu ambaye haamini alicho kiona.

“Shem”

“Mmm”

“Tuondoke”

“Sa….wa sawa”

Shemeji alipatwa na kigugumizi.

“Madogo now nina elekea Muhimbili, nani ata niletea gari?”

“Nitalileta mimi, nitampitisha Maulid kwake kisha nita lileta huko, una hitaji saa ngapi?”

“Saa mbili hivi usiku”

“Sawa”

Nikabidhi Judy bastola kisha nikaingia katika gari la shemeji na kuondoka kituo hichi cha polisi.

“Shemeji”

“Naam”

“Samahani lakini”

“Bila samahani”

“Wale vijana mbona waa kuita wewe mkuu. Kwani wewe ni nani?”

“Mimi ni muendesha taksi, masikini na kapuku wa kawaida sana”

Kauli yangu ikamfanya shemeji kukaa kimya kwa maana maneno hayo ya masikini na kapuku yeye na wana familia wake huwa wana penda kuniita sana.

“Samahani shemeji kwa kila jambo lililo tokea”

“Usijali nimesha wasamahe kwa maana hamjui mulitendalo. Ulicho kiona pale polisi, na nilicho kifanya funga kinywa chako na usimueleze mtu yoyote. Tuna elewana”

“Ndio shemeji”

Hakika leo shemeji yangu ame kuwa mpole na mnyenyekevu. Tukafika hospitali ya Muhimbili, ndugu zake walipo tuona tume ongozana nao wenyewe wakajawa na mshangao. Cauther akanikimbilia na kunikumbatia kwa nguvu.

“Vipi hali ya baba?”

“Tuna mshukuru Mungu ame zinduka na tume weza kuzungumza naye”

“Ni jambo la kumshukuru Mungu kwa kweli”

“Yaa vipi mbona ume ongozana na adui yako?”

“Mimi sina uadui na mtu yoyote wa familia yako mke wangu”

“Ila Salumu huwa ana kuchukia sana”

“Yaa nalifahamu hilo, ila naona nyota zimeendana leo”

“Ehee ana semaje kuhusiana na swala zima wale majambazi?”

“Ana dai ni wafanya biashara wezake ila kwa sasa wapo polisi wamesha kamatwa”

“Umewakamata wewe?”

“Yaa nimeshirikiana pamoja na Judy na Maulid”

“Wale wa jana?”

“Yaaa”

“Nashukuru sana mume wangu japo najua nime kuingiza kwenye matatizo ambayo huku paswa kuingia kwa sasa”

“Usijali ni jukumu langu. Ila Ukitazamia hali ya baba ipo vipi?”

“Hadi ana zungumza ni jambo la kumshukuru Mungu. Madaktari wana sema risasi yake alizo pigwa hazikuleta madhara yoyote kwenye vitu vya ndani ya mwili wake.

“Ahaa sawa sawa. Vipi tuta rudi hotelini leo?”

“Yaaa, now nina amani”

“Shemeji njoo tujumuike na familia bwana”

Salumu alizungumza huku akinishika mkono na kunivuta hadi katika benchi walilo kaa ndugu zake.

“Kaa hapa bwana. Usisisimame simame kule”

Ndugu wa mke wangu wakazidi kushangaa. Mama mkwe akamuuliza kwa lugha ya kiarabu Salumu wakihisi kwamba sifahamu lugha hiyo, kumbe nina ijua vizuri.

“Mbona leo una mkarimu sana huyu masikini?”

Mama Cauther alizungumza kwa kiarabu.

“Mama shemeji hapa ndio aliye wakamata majambazi walio mpiga risasi baba. Na sasa hivi wapo polisi”

Salumu alijibu kwa kiarabu na kuwafanya watu wote kunitazama kwa maana walikuwa wana nichukulia ni mnyonge nisiye weza kufanya jambo lolote.

“Una tudanganya kaka”

Mdogo wao wa mwisho alizungumza kwa kiarabu.

“Haki ya Mungu vile. Nimeshuhudia kwa macho yangu shemeji ana piga ngumi kama vile Jet Lee”

Salumu alizidi kunipa sifa mbele ya ndugu zake kwa lugha yao ya kiarabu. Mke wangu akawa na kazi ya kunishika kiganja changu cha kulia huku akiniminya minya.

“Muendesha taksi na kupigana wapi na wapi. Umechanganyikiwa na wewe ehee?”

Shangazi yao alizungumza kwa lugha hiyo.

“Mke wangu tuna weza kuondoka”

Nilimnong’oneza Cauther sikioni mwake kwa maana mazungumzo haya yanaweza kunikera.

“Ngoja niwaage”

Simu yangu ikaanza kuita, nikaitoa mfukono na kukuta ni namba ya Judy. Nikasimama na kupiga hatua kadhaa kisha nikaipokea.

“Dogo”

“Mkuu nipo nje hapa”

“Sawa nina toka muda si mrefu”

“Vipi kuhusiana na yule RPC umemripoti?”

“Achana naye yeye mwenyewe ata jiripoti”

“Sawa mkuu”

Nikakata simu na kurudi eneo walipo wana familia wa mke wangu.

“Ninaomba munisikilize. Musipende kumdharua mtu msiye mfahamu kwa kumuangalia usoni mwake na kumuangalia kazi yake anayo ifanya. Watu wana maisha mazuri kuliko hayo munayo yadhania nyinyi. Nimemsaidia baba mkwe kwa sababu ni mke wangu na musipende kuwaona watu weusi hawana uwezo wa kufanya jambo lolote ikwa nyinyi nanyi muna isha kwenye nchi ya watu weusi na muna shuhudia jinsi nchi yetu inavyo kwenda hivyo tusidharauliane”

Nilizungumza kwa kiarabu na kuwafanya ndugu wote wa Cauther kustuka kwa maana walihisi kwamba sifahamu kiarabu wanacho kizungumza. Nikamshika mkono Cauther anaye tabasamu kwa furaha na taratibu tukaanza kuondoka eneo hili nikiamini kwamba leo hii ndugu wa Cauther wamesha pata picha kwamba mimi ni mtu wa aina gani.

“Baby yaani leo umenifurahisha sana. Yaani umewakata kata kidomo hususani Shangazi anaye jifanya ana ropoka kama emenizaa yeye”

“Dawa ya jeuri ni jeuri tu”

Tukafika eneo la maegesho, Judy akasalimiana na mke wangu.

“Ehee dogo vipi ume kuja na usafiri wako?”

“Hapana ila ningependa leo mukapafahamu kwangu, nime andaa chakula cha usiku kwa ajili yenu”

“Waooo hilo ni jambo zuri mume wangu. Twende tu wifi”

Cauther alizungumza kwa furaha na tukaianza safari ya kuelekea nyumbani kwake. Tukafika majira ya saa mbili usiku, tukapata chakula cha usiku huku tukizungumza mambo mengi kusiana na maisha na wakati huu nikazidi kumfahamu Judy kwa pamoja.

“Mkuu”

Judy aliniita kwa sauti ya upole mbele ya mke wangu mara baada ya kumaliza kula.

“Ndio dogo”

“Nime furahi sana kufanya kazi na wewe. Hata Mulid naye ame furahi kufanya kazi nawe. Tuna kuomba kwa pamoja mimi na Mulid tafadhali tuna kuomba urudi kazini. Nime weza kusikia historia yako uliyo tuadithia tukiwa kwenye ndege. Ila kama unavyo jua kwamba maisha yetu yametolewa kuilinda nchi na watu. Kufa kwetu ni jambo la kawaida sana. Nina kuomba sana ikiwezekana uunde kikosi kingine cha X. Mimi na Maulid tupo tayari kujumuika nawe kwenye kikosi hicho”

Judy alizungumza kwa upole na kunifanya nishushe pumzi, nikamgeukia mke wangu ambaye naye amenitazama pasipo kuzungumza chochote.

“Wifi, kwa niaba yangu nina kuomba uniombee kwa mkuu hapo, aweze kurudi kazini bado tuna muhitaji sana”

Taratibu mke wangu akanishika viganja vya mikono yangu kisha akanitazama usoni mwangu.

“Mume wangu”

“Naam”

“Laiti ingekuwa si wewe na vijana wako, nina imani hadi sasa majambazi wasinge kuwa wame kamatwa na kama ni watu walio kuwa karibu na kaka sijui ni kitu gani wangemfanya. Kwa moyo mmoja nina Kurusu mume wangu urudi kazini, nipo tayari kukubaliana na hali yoyote itakayo jitokeza kwenye kazi zako. Nina kuomba sana mume wangu urudi kazini”

Mke wangu alizungumza kwa hisia kali sana huku machozi yakimlenga lenga usoni mwake. Taratibu nikasimama huku nikimtazama mke wangu na Judy katika nyuso zao. Katika maisha yangu sikufikiria kurudi katika kazi yangu ua ujasusi ambayo ni hatari sana kwa maisha yangu na maisha ya mke wangu. Na hata kama mke wangu ame nikubalia nirudi kazini ila bado hajakumbana na hatari ambayo ita mfanya asitamani kuniona tena nikiwa nina ifanya kazi hiyo.


“Judy”

“Ndio mkuu”

“Nina kuomba nikuache ngoja sisi turudi hotelini. Cauther nyanyuka twende”

“Ila mume…..”

“Nyanyuka twende”

Nikamkazia sura Cauther na taratibu akanyanyuka kwenye kiti chake na tukaondoka nyumbani hapa kwa Judy. Ukimya ukatawala ndani ya gari huku akilini mwangu nikikumbuka namna jinsi rafiki zangu walivyo uwawa nchini Pakistani kikatili sana nikiwa nina shuhudia kwa macho yangu na nikashindwa kuwasaidia. Jasho likaanza kunichirizika usoni mwangu, hofu nayo ikazidi kunitawala kiasi cha kujikuta nikianza kuyumbisha gari.

“Baby una fanya nini?”

Cauther aliniuliza huku akinistua.

“Ehee?”

“Gari ina hama barabarani”

Nikaliweka gari sawa, kisha taratibu nikapungua mwendo na kusimama kabisa pembezoni mwa barabara.

“Endesha”

Nilizungumza huku nikihamia siti ya nyuma. Hali hii mke wangu hakuwahi kuniona nayo toka nimewahi kuwa naye. Akanitazama kwa sekunde kadhaa kisha akahamia kwenye siti ya dereva na tukaendelea na safari.

“Mume wangu kama nime kukosea nina kuomba unisamehe sana”

“Hujanikosea”

“Nime kukosea labda kukuomba urudi kazini”

Nikarudi na kukaa siti ya mbele pembeni na mke wangu. Tukafika hotelini hapa ambapo tuna siku kadhaa za kuishi eneo hili. Tukashuka kwenye gari letu na kuingia chumbani, nikaa kwenye moja ya sofa huku mikono ikinitetemeka hadi nikaanza kujishangaa. Picha za rafiki zangu zikaanza kunijia katika ufahamu wangu wa akili.

“Mume wangu”

Cauther aliniita huku akiwa amepiga magoti mbele yangu.

“Mmmm”

“Una tatizo gani au una umwa?”

“Haa…hahaa..hapa”

Nilijibu kwa woga mwingi sana. Amani ndani ya moyo wangu imenipotea kabisa kiasi cha kushindwa kujua nina fanya nini. Mke wangu akanitazama kwa sekunde kadhaa kisha akanishika mashavu na viganja vyake viwili.

“Mume wangu toka nijuane nawe sija wahi kukuona ukiwa katika wakati kama huu. Tafadhali ni na kuomba uniambie nini kina kusumbua?”

“Yaani nikiwazia swala la kurudi kichwani nina kumbuka maiti za rafiki zangu walio uwawa mbele ya macho yangu nikiwa nina shuhudia na sikuwa na uwezo wa kuwasaidia mke wagu. Tulikuwa na melengo mengi sana na rafiki zangu hao kwa maana kuna kipindi tulikuwa na ndoto za kuanzisha shirika kubwa la kijasusi kama yalivyo mashiriki mengine makubwa ya usalama duniani.”

Nilizungumza kwa sauti ya unyonge kiasi cha kumfanya mke wangu kunionea huruma.

“Pole mume wangu kwa ajili ya rafiki zako.”

“Ndio maana mke wangu sitaki kabisa kujihusisha na mambo ya kiserikali. Ipo siku nita kufa alafu wewe na wanangu muta ishi maisha ya tabu sana”

“Nime kuelewa mume wangu, sinto hitaji kukuomba tena juu ya hili jambo. Utakapo ridhia kurudi ni sawa ila usipo ridhia kurudi kazini pia ni sawa”

“Hadi kesho kama hali ya baba ita kuwa ina nafuu basi tuta kwenda nchini Brazili kwa ajili ya mapumziko”

“Kweli baby?”

“Yes honey tuta kwenda nchini Brazili ukashangae shangae shangae mabichi makubwa duniani”

“Hahaa kwani wewe mume wangu umesha wahi kwenda?”

“Yaa kipindi nilipo na timu yangu, kipindi cha likizo basi tuna kwenda huko kwa ajili ya kula bata”

“Kama nina waona vile”

“Yaaa”

Mke wangu akanikalia mapajani mwangu huku akinitazama kwa macho yaliyo jaa mahaba tele. NIkaanza kumpapasa kiuno chake taratibu sana, hisia za mapenzi zikatawala kati yetu. Hapakuwa na haja ya kupanda kitandani na shuhuli nzima ya kuburudishana tukaimalizia katika sofa hili huku kila mmoja akimfurahia mwenzake katika tendo hili.

“Alafu nilikuwa nimesahau jambo moja mke wangu?”

“Jambo gani?”

“Nahitaji kutazama malipo niliyo lipwa na serikali katika oparesheni ya kumuokoa raisi”

“Wamesha kulipa?”

“Yaaa, ila kwenye akaunti yangu ya kazi ambayo kwa kipindi cha nyuma malipo yangu yote ya kazi nilikuwa nina lipwa huko”

Nikaingia kwenye akaunti yangu hii ambayo ni mara chache sana huwa nina ifungua kutoa pesa.

“Wooo”

“Wmekuingizia kiasi gani?”

“Dola milioni moja pointi tano”

“Ohoo mume wangu si pesa nyingi hizo?”

“Yaa ila kazi niliyo ifanya ni kubwa sana mke wangu. Una jua raisi n dio kila kitu kwenye hii nchi so anapotekwa kuna mambo mengi sana yapo hatarini ambayo magaidi wana weza kuyatumia”

“Mambo gani hayo mume wangu?”

“Mmmm moja ni swala zima la kisilaha. Una jua nchi yetu ina visima vya kuzalishia mabomu ya nyuklia. Password za kulipulia mabomu hayo ana zifahamu raisi na makamu wake tu. Sasa endapo raisi akaminywa na akazitaja uje kuna hatihati mbaya sana ya matatizo kutokea.”

“Okay hapo nime kuelewa”

“So hapa kiasi changu cha pesa ni dola milooni kumi. Kabla ya kwenda Brazil nita kupeleka Makete kwenye kituo cha watoto yatima. Nahitaji tukatoe msaada kwa watoto wengine”

“Ni jambo la hari mume wangu”

“Unajua kuna kipondi nilitaka kuzitoa pesa zote kwa watoto wale. Ila nilipo kuja kugundua kuna wapiga madili pale, nikasitisha zoezi hilo. Ila hivi sasa kama nikitoa hata shilingi mia moja yangu ni lazima nita ifwatilia nihakikishe na kufahamu kwamba ime kwenda wapi na imefanyia nini”

“Haya hilo ni jambo jema mume wangu”

Mke wangu alizungumza huku akinikumbatia kwa furaha sana.

***

Baada ya siku mbili hali ya baba mkwe ikaimarika na daktari akatuhakikishia kwamba ndani ya siku nne zijazo wata mruhusu kutoka hospitalini hapo. Siku iliyo fwata tukaianza safari ya kuelekea mkoani Iringa mimi na mke wangu. Safari ya milima mabonge na kona nyingi na umbali wa kilomita 488.7 ikatugarimu masaa nane na dakika zake kwa maana kuna wakati niliendesha gari kwa kasi sana, tofauti na jinsi madereva wa mabasi ya abiri wanavyo paswa kuendesha magari yao.

“Kuna baridi”

Mke wangu alizungumza huku akiwa amejikunyata. Nikafungua mlango wa nyuma wa gari langu na kumtolea koti moja kubwa na kumvisha. Tukaingia eneo la kituo hichi ambacho kime badilika kwa asilimia kadhaa. Watu wengi wana tushangaa sana kwa maana wengi wana niona ni mgeni. Nikaelekea katika ofisi za utawala, nikakutana na bibi Esturida, bibi ambaye alitulea mimi na wezangu toka tukiwa watoto. Akanitazama kwa sekunde kadhaa kisha akasimama huku akijaribu kuvuta kumbukumbu. Taratibu nikatabasamu huku nikimtazama.

“Eddy”

Alitiita huku akionekana kuto kuwa na uhakika na jina langu.

“Ndio bibi ni mimi”

Kwa kasi ya ajabu bibi Esturida akanikimbilia na kunikumbatia kwa nguvu huku akilia kwa uchungu sana. Nikakumbatiana kwa dakika mbili, kisha nikamuachia.

“Umekuwa mkubwa sana”

Bibi Esturida alizungumza huku akinitazama kuanzia juu hadi chini.

“Nashukuru”

“Wezako wapo wapi?”

Bibi Esturida aliniuliza huku machozi ya furaha yakimwagika usoni mwake.

“Wapo”

Ilibidi nimdanganye kwa maana umri wa mwana mama huyu ambaye ndio alite tulie ume kwenda sana.

“Ehee huyu ni nani yako?”

“Huyu ni mke wangu”

“Waooo hongera sana Eddy”

“Nashukuru sana bibi yangu”

“Karibini mukae”

Akatukaribisha kwa furaha na tukakaa kwenye viti hivyi vilivyopo ofisini kwa Esturida.

“Haki ya Mungu nime kuza. Eddy toka nilipo kuokota kachanga hadi ume kuwa mbaba na una mke kwa kweli Mungu ni mwema”

“Ni kweli bibi. Mke wangu ana itwa Cauther”

“Karibu sana Cauther. Hapa ndipo nyumbani kwa kina Eddy na wezake wote.”

“Nashukuru sana bibi”

“Na mimi ndio niliye muokota kipindi hicho akiwa mchanga, yaani wa kulia ng’aa ng’aa”

Sote tukajikuta tukicheka kwa furaha.

“Walikuwa niwatundu sana. Yaani hadi wame toroka, walitupa shida nyingi sana kumtafuta ila mwishowe hatukufanikiwa. Ila jambo la kumshukuru Mungu sasa wamekuwa na kuwa watu wazima”

“Ni kweli bibi”

“Ehee una fanya kazi gani siku hizi?”

“Mfanya biashara, leo nime kuja kutoa kitu kidogo kwa ajili ya wezetu hawa.”

“Mungu ashukuriwe, na hilo ndio tunalo waombea munapo fanikiwa muweze kukumbuka nyumbani mulipo toka”

“Ni kweli bibi. Nanao sura mpya za walezi wale wengine wapo wapi?”

“Wengine waliachana na kazi. Wengine wame fariki kwa maana miaka thelathini na moja sio haba, ni kwa rehema ya Mungu tu umeweza kunikuta nikiwa hai”

“Ni kweli bibi”

Tukaanza kutembezwa kwenye kituo hichi.

“Huu uwanja mkubwa hapa muna lengo nao gani?”

“Huu upo tu kama unavyo uona”

“Mke wangu una onaje hapa tukajenga gorofa kama tano za mabweni ya watoto?”

“Ni jambo jema mume wangu”

“Ngoja kwanza Eddy. Una sema kweli una jengo hizo gorofa?”

“Ndio bibi, hapa ni nyumbani kwangu na ni lazima nijenge”

Bibi Esturida akajawa na furaha sana. Akaandaa kikao na bodi ya chuo hichi, tukapanga namba mabweni hayo yatakavvyo tengenezwa. Siku hii hii akatafutwa Mkandarasi, nikamueleza ni namna gani ambavyo nina hitaji mabweni hayo yajengwe. Akatuahidi siku inayo fwata ata tuletea ramani. Usiku wa siku hii ya leo nika fanya sherehe kubwa kituoni hapa ya kumshukuru Mungu kwa kuweza kulelewa hapa kwani laiti ingekuwa si kuokotwa na bibi Esturida nisinge kuwa hai hadi sasa kwa maana baridi inge niua. Watoto wengi wakajawana furaha sana katika sherehe hii.

“Bibi”

Nilimuuita bibi Esturida huku tukitazama maonyesho ya maigizo ya watoto hawa.

“Ndio Eddy”

“Katika siku zote hukuwahi kusikia mwamamke yoyote akitafuta mwanaye aliye mtupa katika ule mtaro?”

“Kwa kweli sija wahi kusikia, japo ile siku nilipo kuokota niliweza kuulizia maeneo ya jirani kwamba ni nani ambaye ame mtupa mtoto wake ila sikuweza kupata jibu sahihi”

“Sawa sawa bibi”

“Ila Mungu ni mwema, tazama leo una maisha yako. Hakikisha una kuwa baba bora kwenye familia yako na mume bora. Kwa maana ukiona mwanamke ana telekeza mtoto na kumtupa kwenye virambo ina maana kuna mambo mawili. Moja mwanaume aliye zaa naye hakuwa sahihi, au alikuwani mwanafunzi ambaye alipatia ujauzto shule hivyo akaona atoe mimba kisiri na kukutupa mtaroni. Katika miaka ile ya zamani watu wengi walikuwa wana tupa sana watoto kutokana na maisha magumu. Hata wale wezako ulio toroka nao, nao ni hivyo hivyo nilikuwa nina wakuta katika mazingira tofauti tofauti ambayo ni hatarishi.”

“Nina kushukuru sana kwa wema wako. Nakuombea kwa Mungu azidi kukupa maisha marefu zaidi ya hapa ulipo”

“Amen”

Baada ya sherehe hii, tulakaelekea nyumbani kwa bibi Esturida. Tukalala nyumbani kwake hadi siku iliyo fwata, tukakutana na mkandarasi, akatukabidhi ramani hiyo iliyo pitishwa mbele ya bodi ya kituo hichi. Nikamlipa mkandarai cheki ya bilioni moja nukta tano ya Kitanzania. Nikamsisitizia mkandarasi kujenga jengo lenye ubora na kama akijenga jengo lililo chini ya kiwango basi ata lipa kiasi hicho cha pesa.

“Eddy”

“Ndio bibi”

“Nina omba namba za wezako kwa maana ni muda mrefu sana toka muondoke. Ninge penda niweze kuzungumza nao na kufahamu hali zao.”

Maneno ya bibi Esturida yakanifanya mimi na mke wangu Cauther kutazamana kwa maana endapo nita muambia bibi yangu huyu kwamba vijana wake watatu alio tuliea na kutupenda wamefariki dunia na kwa sasa hatupo nao tena.



“Amen”

Baada ya sherehe hii, tulakaelekea nyumbani kwa bibi Esturida. Tukalala nyumbani kwake hadi siku iliyo fwata, tukakutana na mkandarasi, akatukabidhi ramani hiyo iliyo pitishwa mbele ya bodi ya kituo hichi. Nikamlipa mkandarai cheki ya bilioni moja nukta tano ya Kitanzania. Nikamsisitizia mkandarasi kujenga jengo lenye ubora na kama akijenga jengo lililo chini ya kiwango basi ata lipa kiasi hicho cha pesa.

“Eddy”

“Ndio bibi”

“Nina omba namba za wezako kwa maana ni muda mrefu sana toka muondoke. Ninge penda niweze kuzungumza nao na kufahamu hali zao.”

Maneno ya bibi Esturida yakanifanya mimi na mke wangu Cauther kutazamana kwa maana endapo nita muambia bibi yangu huyu kwamba vijana wake watatu alio tuliea na kutupenda wamefariki dunia na kwa sasa hatupo nao tena.


ENDLEA

“Bibi?”

“Niambie Eddy”

“Kuna long story imeweza kutokea katika miaka hii mitatu na nusu iliyo pita sasa”

Nikakaa chini na bibi Esturida na kumueleza kuanzia siku tulipo toroka katika kituo hichi hadi siku nilipo wapoteza wezangu. Bibi Esturida akamwagikwa na machozi mengi sana kwa maana stori hiyo ime muumiza sana moyo wake.

“Ndio maana hichi nilicho kipata kwenye masisha yangu nina kigawa kwa ndugu zangu hawa”

“Mungu azidi kukubariki mwanangu na nina kuombea uzidi kufanikiwa”

“Nina shukuru sana bibi”

Nikaacha kiasi chamilioni kumi kwa ajili ya kununualia chakula cha watoto wote kisha tukaanza kurudi jijini Dar es Saalam.

“Baby”

“Niambie mke wangu”

“Kwa kweli nime furahisana kukutana na wale watoto”

“Mungu awarehemu kwa kweli kwa maana maisha bado ni bila bila”

“Ni kweli mume wangu”

Tukafika jijini Dar es Salaam majira ya saa kumi usiku, hatukurudi hotelini na moja kwa moja tukaelekea nyumbani kwetu maeneo ya Kawe, tulipo panga katika nyumba ya vyumba viwili, seble na jiko.

“Uhuu nime pamiss sana kwangu”

Cauther alizungumza huku akijitupa kwenye moja ya sofa lililopo hapa sebleni.

“Nimechoka sana, mke wangu”

“Hata mimi nimechoka kwa kweli, safari ni ndefu sana mume wangu”

Simu yangu ikaanza kuita,nikaitoa mfukoni, nikastuka sana mara baada ya kukuta namba hiyo inayo piga in code maalumu kutoka ikulu.

“Mbona hupokei baby ni nani huyo?”

Cauther alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.

“Hii ni namba kutoka ikulu”

“Pokea sasa baby ina weza kuwa ni muhimu”

“Sasa hivi ni usiku sana mke wangu hadi nina tafutwa ujue simu hii sio salama”

“Pokea tu honey”

Nikaipokea simu na kuiweka sikioni mwangu.

“Haloo Eddy, raisi hapa”

“Nina ifahamu sauti yako muheshimiwa. Habari yako”

“Salama ila sio salama, kuna tatito kubwa sana la kiusalama tuna kuomba sana uweze kufika ikulu sasa hivi”

“Sasa hivi?”

“Ndio”

Simu ikakatwa na kujikuta nikishusha pumzi huku nikimtazama mke wangu.

“Kuna nini mume wangu?”

“Muheshimiwa raisi ameniita ikulu. Anadai kuna tatizo kubwa la kiusalama lime weza kutokea”

“Mmmmm”

“Ndio maana sikuhitaji kuipokea simu”

“Nenda tu ukasikilize mume wangu”

“Nikikuacha peke yako uta huto ogopa?”

“Jamani baby ni mara ngapi ume kuwa ukiniacha nyumbani peke yangu ukiwa una kwenda kukesha barabarani. Wewe nenda, ila ukifika naomba unifahamishe kama ume fika”

“Sawa mama watoto”

“Nikambusu mke wangu mdomoni mwake kiha nikaondoka nyumbani hapa na kuelekea ikulu. Nikafika ikulu na nika ruhusiwa na walinzi ambao wamepewa maagizo ya mimai kufika ikulu. Nikashuka kwenye gari kisha nikaongozana na mlinzi hadi katika ukumbi wa kuongozea oparesheni za usalama ambao upo chini ya ikulu. Nikakutana na wakuu wa majeshi na nyuso za watu wengi ndani hapa zime jawa na majonzi mengi kiasi cha kunifanya nijiulize maswali mengi. Nikasalimiaa na muheshimiwa raisin a akanikaribisha kwenye kiti kilicho wazi nami nikaka. Nikazungusha zungusha macho yangu ndani hapa ila sikuweza kumuona makamu wa raisi.

“Tuna weza kuendelea sasa?”

Raisi alizungumza huku akitutazama watu wote tulio kaa kwenye meza hii.

“X kwa harakaharaka ni kwamba kume tokea shambulizi kwa wanajeshi wetu wanao lina usalama katika nchi ya Congo. Wanajeshi wapatao thelathini na sita wameweza kuuwawa usiku huu, huku wanajeshi kumi na mbili wakiwa ni kutoka nchini Tanzania na wengine ni kutoka nchi za Congo, Kenya na Uganda”

Nikastuka kidogo huku nikigeuzia macho yagu kwenye tv kubwa iliyo jaa ukuta mzima wa ukumbi huu, ikionyesha miili ya wanajeshi walio uwawa.

“Shambulizo hilo lime wahusisha waasi wa Yakutumba wakishirikiana na waasi kutoka nchi jirani ya Burundi wa FLN(National Liberation Front)”

Raisi akanyamaza kidogo kisha akaendelea kuzungumza.

“Tukiwa kama chi washirika, tunao toa vikosi vyetu kwenda kutetea amani za nchi yao, hatuwezi kukaa kimya. Ni lazima tuhakikishe kwamba tuna visambaratisha vikosi hivi. Iwe ni angani, majini au nchi kavu ni lazima tita wasambaratisha”

Raisi alizidi kuzugumza kwa uchungu sana. Macho yangu bado yanaendelea kutazama maiti za wamajeshi hao ambao wana onyesha wameshambuliwa kwa mabomu ya kustukiza.

“X upo nasi?”

Mkuu wa jeshi aliniuliza huku akinitazama.

“Ndio”

“Muheshimiwa amesemaje?”

Swali la mkuu huyu wajeshi likawafanya watu wete kumtazama.

“Nina imani amenisikia”

Raisi alizungumza na kumfanya mkuu wa jeshi kunitazama kwa macho makali yanayo dhiirisha kwamba ana chuki kidogo namimi ambayo sifahamu ni nini chanzo chake.

“Habari za hadi sasa hatujajua ni jinsi gani waasi hao walivyo weza kufanya shambulizi hilo la kustukiza. X tunacho kihitaji ni wewe kuelekea nchini Congo, ukiongozana na makamu wa raisi kwenda kuonana na raisi wa nchi hiyo pamoja na wakuu wa jeshi kupanga namna mpya ya kupambana na waasi hao.”

“Safari ni lini?”

“Saa kumi na mbili alfajiri, mutaondoka na ndege ya kijeshi kuelekea nchini DRC. Utakuwa ni miongoni mwa walinzi wa siri wa makamu wa raisi na pia uta utakuwa mshauri wake. Tumeelewana X?”

“Nime kuelewa muheshimiwa”

“Kitambulisho chako chakazi kipo tayari. Uta pita pale kwa Maria ata kukabidhi kila kitu chako. Tuna tambua kwamba upo honeymoon ila bado una hitajika kwa ajuli ya taifa hili”

Raisi alizungumza huku akinitazama usoni mwanagu kwa namna moja ama nyingine ana tambua kabisa kwamba sija furahishwa kurudi kazini.

“Sawa”

“Ila muheshimiwa raisi huyu kijanaa uso wake una onyesha dhairi kwamba haja kubaliana na kazi hiyo. Mbona kuna vijana wengi na wenye uwezo kuliko yeye. Kwa nini achukuliwe yeye tu?”

Mkuu wajeshi alishauri hadi watu wote tuka mtazama.

“Una mjua X?”

Raisi alimuuliza mkuu wamajeshi, akakaa kimya akimaanisha kwamba hanijui.

“Sikatai kwamba kuna vijana wana uwezo, ila X na wezake ambao kwa sasa hawapo duniani, Mungu azilaze pema roho za marehemu, ndio watu pekee ambao walipata mafunzo mengi kupita maelezo, mafunzo yaliyo wapa ujuzi mkubwa kuliko unavyo fikiria na wamefanya oparesheni nyingi zilizo fanikiwa na katika oparesheni mia tao na kumi, ni oparesheni mia tatu na tisa zilfanikiwa na moja ya mia tatu na kumi ikafeli na wezake wakauwawa. Juzi amekamilisha oparesheni yake ya mia tatu na kumi na moja ya kuniokoa mimi na watu wangu, nyote katika hichi chumba mulishuhudia uwezo wake na pia muliona alivyo jitahidi kuwaokoa vijana ambao nyinyi muliwaita ndio the best comandoo ila mwishowe waliingia mikooni mwa adui. So jenerali kabla ya kuzungumza chunguza unacho kizungumza kwa maana nime ona una wivu wa kijinga ndani yako. Wapeni mafunzo vijana wenu tupate the best kama hawa. Hawa ndio zao la mwisho la vijana wa makamu wa raisi kipindi alipo kuwa amekalia hicho kiti chako cha ujenerali na toka uchukue kiti chake ni nani ambaye ume mtoa na akawa the best sectrety weapon?”

Raisi alizungumza kwa msisitizo na ukali kidogo huku akimtazama jenerali kwa macho ya ukali.

“X nenda kajiandae na nyumbani kwako uta wapeka sectert service wanne kwaajili ya kumlinda mke wako hadi utakapo rudi kwenye hii oparesheni”

“Nashukuru mkuu”

Nikasimama huku nikimkonyeza jenerali wa jeshi. Nikapita kwa Maria secretary wa raisi kwa sasa.

“Jamani Eddy mambo?”

Maria alinisalimia kwa bashasha zote.

“Safi naona una zidi kuwa mzuri, mtoto dimpozi zime bonyea bonyea?”

“Hahaa bado huja acha masihara yako Eddy”

“No sio masihara, ila nina kueleza ukweli wewe mzuri. Vipi umesha olewa?”

“Bado si nilikuwa nina kusubiria wewe unioe, ila nikasikia kwamba ume oa na leo nakuona una pete kidoleni”

“Ndio nimesha oa mwenzako, mtoto wa kiarabu kutoka huko Oman. Ila poleni kwa kuwapoteza wezenu”

“Tumesha poa na shukrani bwana kwa kutusaidia ile siku. Kwani tulisha kata tamaa ya kuishikabisa”

“Ila ujue wewe ni jasiri kwamaana tukio limetokea last week,leo upokazini?”

“Unajua ukisha kuwa katika nafasi kama hii basi una paswa kuwa tayari kwakila jambo. Vitu vyako hivi hapa, kitambulisho cha usalama , simu, na your baby”

Maria alizungumza kwa utani huku akikabidhi bastola iloyomo ndani ya kifuko maalumu.Nikaichomoa bastola hiyo na nikaikoki vizuri.

“Yee kweli hii ni my baby, ume juaje nina penda bastola hizi”

“Ningekuwa sikujui hapo sawa. Ila kwa miaka mitatu tuliyo fanya kazi niliweza kukufahamu vizuri sana”

“Haya bawana alafu nilikuwa nime sahau kukuuliza jambo”

“Jambo gani?”

“Hivi Catherine amesha zikwa?”

“Yaa alisha pelekwa kwao Bukoba. Aisee nilimshuhudia akiuwawa mbele yangu, niliogopa sana yaani asikuambie mtu”

“Niliiona ile video. Iliniumiza sana na ndio aliye nifanya nikubali kurudi kazini japo ilikuwa ni siku yangu ya harusi”

“Daa sitaki kuyakumbuka hayo Eddy. Yananiumiza moyo wangu sana”

“Mungu amlaze mahali pema peponi”

“Amen. Alafu Eddy, Mungu bariki ukifanikiwa kurudi kutoka DRC nahitaji tupate muda mchache wa mimi na wewe kuzungumza jambo”

“Jambo la heri au?”

“Ni la heri si una juaga mimi sinaga shari”

“Mmm okay, ngoja nimuwahi mke wangu bwana nika pige mechi ya mwisho mwisho, sasa hivi ni saa kumi, kimoja tu kina nitosha”

“Angalia usije uka chelewa?”

“Sichelewagi mimi”

Nikaachana na Maria ambaye uso wake umejawa nafuraha sana kuniona, nikakutana na walinzi wanne wa ikulu ambao nime kabidhiwa kwa ajili ya kulinda nyumbani kwangu. Tukaondoka huku mmoja akiwa amepanda katika gari langu na watatu wakiwa wamepanda katika gari lao. Tukafika nyumbani kwangu, nikafungua geti kwa funguo yangu ya ziada na tukaingia ndani.

“Hei baby”

Nilimuita Cauther dirishani.

“Mmm”

“Amka nime rudi”

Baada ya dakika mbili mke wangu akanifungulia mlango, akachungulia watu nilio ongozana nao.

“Hawa ni kina nani mume wangu?”

“Walinzi wako, tuingie ndani tukazungumze”

Nikawaacha walinzi nje na sisi tukaingia ndani, nikamueleza mke wangu kila kitu kilicho tokea na kumfanya ajawe na uso wa huzini.

“Kwa hiyo ume kubali kwenda?”

“Ninge fanyaje mke wangu, ndo maana nili kuambia kwamba sihitaji kurudi kazini kwani madhara ndio kama haya”

“Eddy”

“Naam”

“Kuwa makini mume angu huko unapo kwenda. Tambua kwamba nina kuhitaji”

“Usijali mke wangu”

Nikatazama saa ya ukutani na nikaona nina muda wa kutosha. Nikamnyanyua mke wangu na kuingia naye chumbani, nikamlaza juu ya kitandaa na kuanza kumpa penzi la haraha haraka. Ndani ya dakika kumi na tano tukamaliza mzunguko mtanange huu ambao ni mfupi na mkali sana.

“Asante mume wangu”

“Asante nawe mke wangu kipenzi”

Tukaoga kwa pamoja, kisha mke wangu akaniandalia nguo haraka haraka.

“Nimeshau kuuliza mume wangu. Muna kaa kwa muda gani?”

“Sina uhakika ila nikifika huko nita kukuza baby”

“Sawa mume wangu”

Nikajiandaa haraka haraka, tukatoka nje, nikamtambulisha mke wangu kwa walinzi hawa na nika waonyesha eneo zimala nje la nyumbayangu. Tukarudi ndani na mkewangu na nika muingiza katika bafu la chumbani kwangu.

“Kuna sehemu ya siri nahitaji kukuonyesha mke wangu”

“Una maanisha nyeti au?”

“Hahaa sio hivyo”

Nikakito kioo kilichopo bafuni hapa na katika eneo hili la ukuta kuna shelf yangu ya siri ambayo nina hifadhia silaha, vitambulisho vyangu vya zamani vya kazini, hati za kusaifiria pamoja na pesa za kigeni za nchi mbalimbali.

“Endapo kuta tokea tatizo lolote, chukua bastola hii, una ingiza magazine hivi na una vuta hapa mara moja. Hapa uta kuwa ume iruhusu risasi kupanda kwenye chemba tayari kwa kutoka. Uta vuta triga na risasi itatoka. Ume nielewa mke wangu?”

Hembu rudia tena?”

Nikarudia kwa mara ya pili kumuelekeza mke wangu namna ya kuitumia bastola kisha nikamkabidhi na akaanza kufanya kama nilivyo muelekeza. Jambo ambalo nina mshukuru Mungu, mke wangu ana kichwa chepesi sana katika kuelewa mambo.

“Nimeweza”

Mke wangu alizungumza huku akitabasamu sana.

“Okay irudi humu ndani. Utaitumia pale tu kunapo tokea uvamizi, kumbuka hii sio manati, risasi ikitoka na kumpiga mtu sehemu mbaya ana kwenda na maji hivyo kuwa makinimkewangu”

“Nime kuelewa baby. Nipo makini zaidi ya unavyo fikiria”

Nikaitoa magazine pamoja na risasi iliyopo katika chemba ya bastola hii kisha nikairudisha ndani ya shelfu hii. Nikaondoka nyumbani kwangu na kuelekea uwanja wa ndege wa kijeshi. Nikamkuta makamu wa raisi akiwa amesha wasili uwanjani na walinzi wake pamoja na washauri wake kadhaa. Nikasalimiaa naye kisha walinzi wote tunao kwenda kwenye safari hiyo tuka kaa kikao cha dakika kumi kupeana maelekezo ya jinsi gani ambavyo tupasa kumlinda makamu wa raisi katika nchi hatari kama hiyo ya DRC. Baada yakikao hichi kuisha, Judy na Maulid wakanifwata.

“Madogo kumbe tupo pamoja?”

“Ndio mkuu tume furahi sana kukuona hapa”

“Musijali na tambueni kwamba nyinyi ndio watu pekee ninao waamini katika kukamilishahii. Nahitaji twende salama na turudi salama.Maswala ya kutekwa tekwa kitoto kama alivyo tekwa raisi na walinzi wake sihitaji kuyasikia. Tumeelewana?”

“Ndio mkuu”

Nikapeana tano na Judy pamoja na Maulid ikiwa ni ishara kwamba, tutakuwa pamoja kwenye shida na raha ambazo tuta kwenda kukutana nazo kwenye nchi ambayo wanajeshi kumi na mbili wa Tanzania wamevamiwa na kufarik dunia.



Nikamfwata makamu wa raisi ambaye ana jiandaa kwa kuvalia jaketi la kuzuia risasi na hata litokea shambulizo lolote basi haito wedha kuathiria na shambulizi hilo.

“Mkuu katika walinzi wako ni yupi ambaye una muamini kuliko wengine?”

“Ahaa ni yule John na Kane”

“Okay”

“Kwa nini umeniuliza?”

“Kumbuka tuna kwenda nchi ambayo hatujuini nani rafiki kwetu na nani ni adui nawe una fahamu kisa kamili cha raisi hadi kutekwa”

“Yaa hapo nime kuelewa”

“Nashukuru kukuelewa.”

Muda wa kuingia kwenye ndege hii ya kijeshi ambayo imetengenezwa kwa ubaro wa hali ya juu na ina uwezo wa kumlinda makamu wa raisi hewani na kumshambulia adui endapo inapo vamaiwa angani. Saa kumi na mbili alfajiri safari ya kuelekea DRC Congo ikaanza huku kila mtu akiwa amekaa kwenye siti yeka. Nikanyanyuka na kukaa siti ya pembeni mwa makamu wa raisi anaye pitia pitia baadhi ya mafaili.

“Niambie X”

“Kwa mfano raisi wa Congo akakataaa majeshi ya Tanzania kuchukua jukumu la kwenda kushambulia vikosi vilivyo husika na kuwashambulia wanajeshi wetu itakuwaje kwa maana ina bidi tujadili kupata na kukosa?”

“Hilo ni kweli ulilo lizungumza X. Akikataa tuna fanya oparesheni ya kilazima”

“Hili lita leta shida baina ya nchi yake na nchi yetu?”

“Ni kweli ila ina kwa nini akatae ikwa waasi hao tunao kwenda kupambana nao ni kwa ajili ya nchi yake na ni kwa ajili ya kuifanya nchi yake iwe na amani”

“Ila siasa ni kitu kibaya sana”

“Kwa nini una zungumza hivyo X?”

“Yote yanayo tokea katika nchi ya DRC ni kutokana na siasa, madaraka ya mabavu, ufisadi. Endapo nchi inge kuwa na demokrasia hawa waasi wasinge kuwepo. Ila watu wengine wana hityaji kukaa madarakani hadi Mungu awachukue”

“Ni kweli unacho kizungumza. Ila ukija kuyaangalia haya mambo kwa undani sana, uta kuja kugundua kwamba kuna baadhi ya nchi kubwa duniani zina fadhili haya makundi ya waasi kwa kuwapa silaha zenye ubora na wengine kutoa wakufunzi wa kuwafunza hao waasi. Ndio maana uta kuta waasi wana uwezo wa kupambaba na majeshi. Alafu lengo la nchi hizo kubwa zinazo wafadhili hao wapiganaji moja kwa moja wanacho kifanya ni kuchukua mali kama dhahabu na kadhalika. Hivyo katika hili ni lazima tufanye upelelezi wetu kujua ni nani aliye weza kutoa siri hadi kambi ya wanajeshi ikavamiwa”

“Umenikumbusha kitu. Hivi upelelezi ulifanyika juu ya mauaji ya wanajeshi kule Pakistani hadi nikawapoteza wezangu?”

“Nilisikia umoja wa Mataifa waliweza kufanya upelelezi huo. Ila sikupata jawabu kama unavyo jua ni nchi nyingi zilikumba na yale mambo. Labda Mungu akitufanikisha kurudi salama kwenye hii safari uka fwatilie makao makuu ya umoja wa mataifa”

“Nita liangalia hilo kwa jicho la pili”

“Sawa”

Nikarudi kwenye siti yangu na kumuacha makamu wa raisi aendelee na majukumu yake. Nikaitazama pete yangu ya ndoa niliyo ivaa kidoleni. Nikajikuta nikitabasamu huku nikikumbuka maisha yangu ya nyuma jinsi nilivyo kuwa nikijiapisha kwamba sinto kuja kuo siku hata moja, ila viapo vyote hivyo vime yayuka kama barafu. Majira ya saa sita juu ya alama tukatua katika kiwanja cha ndege cha N’djilia Kinsasha Congo. Baada ya ndege kusimama, nikasimama na kuwatazama watu wote ndani ya ndege hiii kwa maana mimi ndio mlinzi mkuu kwa sasa kuhakikisha kwamba makamu waraisi ana kuwa salama katika muda wote tutakao kaa hapa Kinsasha Congo.

“Tumefika. Jukumu letu ni moja tu, kumlinda makamu wa raisi, kuanzia tukishka hapo kwenye ndega na hadi tukapo panda kwenye hii ndege. Naamini kila mmoja earphone yake ipo vizuri”

“Ndio”

“Silaha zenu?”

Kila mmoja akahakika bastola yake na kunidhibitishia kwamba ipo vizuri.

“Bullet proof?”

Kila mmoja ame valia jaketi la kuzuia risasi ndani ya shati lake.

“Miwani?”

Nilizungumza huku nikiwa nime shika miwani yangu nyeusi. Miwani hizi zime tengenezwa maalumu kwa ajili ya walinzi wa raisi, kwani ina uwezo wa kumuona mtu mwenye silaha hata kama amejificha kwenye kundi la watu wengi na ina uwezo wa kumuona vizuri kwa wakati wa usiku hata kama kuna giza nene. Mara baada ya

kuhakikisha kila kitu kwa walinzi wote, nikaruhusu mlango wa ndege hii kufunguliwa huku nikitazama saa yangu ya mkononi na kuhifadhi kichwani muda huu ambao makamu wa raisi ana kwenda kushuka kwenye ndege hii. Nikawa wa kwanza kushuka, nikatazama mandhari ya eneo hili na nikamshuhudia raisi wa DRC pamoja na walinzi wake akiwa amefika kwa ajili kumpokea makamu wetu wa raisi.

Nilipo jiridhisha kwa usalaa ulio imarishwa uwanjani hapa, nikawapa ishara walinzi wezangu na makamu wa araisi akato katika ndege hii na kuanza kushuka kwenye ngazi. Nikawa wa kanza kukanyaga ardhi ya nchi hii ya DRC Congo. Walinzi wengine wanne wakatawanyika na tukamuwe kati makamu wa raisi.

Makamu wa raisi na raisi wa DRC wakapeana mikono na kukumbatiana. Macho yangu yakazidi kuwa makini kwa kila hatua ambayo makamu wa raisi ana piga huku akiwa bega kwa bega na raisi wa nchi hii. Makamu wa raisi akaingia kwenye gari lililo andaliwa kwa ajili yake.

“Judy endesha”

Nilimuambia Judy huku Maulid akikaa siti ya mbele huku nami nikikaa siti ya nyuma pamoja na makamu wa raisi. Walinzi wengine wakaingia kwenye magari mengine na msafara huu ukaanza kuelekea ikulu huku ulinzi ukiwa ni mkali sana.

“Mmmmm karoho kana nienda kasi”

Makamu wa raisi alizungumza na ikabidi nimtazame.

“Kwa nini?”

“Hata sijui, na nikihisi hii hali basi kuna jambo baya lina kuja kutokea”

“Nahitaji walinzi wote muweze kuwa makini”

Niliwasiliana na walinzi wote kwa kutumia kinasa sauti nilicho kibana eneo la kifuani mwangu ndani ya suti yangu.

“Sawa”

Gari hili tulilo panda ni Toyota Land Cruiser V8.

“Hivi hii gari haipitishi risasi kweli?”

Maulid aliuliza.

“Hata sijui kama lime tengenezwa katika ubora huo”

Nilimjibu Mualid huku nikitazama pikipiki ya mbili za polisi zilizopo upande wakulia na kushoto kwetu usawa wa makamu wa raisi.

“Mkuu huu ndio utaratibu wa hapa DRC?”

Nilimuuliza makamu wa raisi na yeye akazitazama pikipiki hizi.

“Sijajua, ila ni pikilipi zilizopo kwenye msafara.”

“John una nisikia?”

“Ndio mkuu”

“Nahitaji gari zetu mbili ziweze kuliweka kati gari la muheshimiwa hao askari wenye pikipiki wasogezeni mbele kwa maana raisi wao hajalindwa na pikipiki”

“Sawa mkuu”

Gari mbili ambazo wamepanda walinzi wa makamu wa raisi, taratibu zikaongeza kasi na kuwafanya askari hawa wenye pikipiki kusogea mbele na gari mbili hizi zikaliweka kati gari la makamu wa raisi, kidogo nikapata amani.Tukafanikiwa kufika ikulu salama salmini. Tukapokelewa vizuri na kabla ya mazungumzo makamu wa raisi na raisi wa DRC wakajumuka katuka kupata chakula cha mchana.

“Mkuu una jihisi njaa?”

Judy alininong’oneza huku tukiwa tumesimama pembeni ya makamu wa raisi anaye endelea kugonga msosi ulio andaliwa.

“Nope akili yangu ina fikiria kikao”

“Sawa mkuu”

“Waambie walinzi wale kwa awamu na hakikisha kwamba hakuna mlinzi anaye kula kupitiliza na kila wanacho kula ni lazima wahakikishe kimepimwa”

Nilimpatia Judy maagizo hayo kwa kumnong’oneza sikioni mwake.

“Sawa mkuu”

Judy akaondoka pembeni yangu na nikaki nikiwa nime simama na John pamoja na Kane ambao wakiwa nchini Tanzania wao ndio walinzi namba moja na mbili wa makamu wa raisi. Baada ya wakuu wetu hawa wawili kupata chakula cha usiku, waka pata muda wa kupiga picha kadhaa kisha ukawadia muda wa kuingia kwenye kikao hichi ambacho kime udhuriwa na raisi, washauri wake wa kiusalama wa nchi ya DR Congo huku nasi kwa upande wetu akiwa ni makamu wa raisi, mimi pamoja na washauri wawili wakamau wa raisi. Walinzi wengine wa makamu wa raisi pamoja walinzi wa raisi wa DR Congo wakabaki nje kuendelea kuimarisha ulinzi.

“Kwanza nipende kutanguliza pole kwa kuwapoteza wanajeshi wako ambao muliwatoa kwa ajili ya kuja kulinda amani katika nchi yangu ila kwa bahati mbaya waka kumbana na kilicho tokea”

“Pole na wewe”

Makamu wa raisi alizungumza huku akimtazama raisi wa DR Congo.

“Nina shukuru sana”

“Kama tulivyo zungumza kwenye simu kwamba leo nita fika na nime timiza ahadi yangu. Dhumuni kuu lililo tuleta hapa ni juu ya waasi ambao wame husika katika kuwaua wanajeshi wetu. Sisi kama nchi ya Tanzania, nchi yenye nguvu Afrika na duniani. Tuna hitaji sasa kupambana sisi kama sisi kuhakikisha kwamba tuna wafyekelea mbali hao maadui zako. Tuna hitaji kuwapiga hadi sebleni kwao, kama alivyo fanya Nduli Idd Amin”

Makamu wa raisi alizungumza kwa msisitozo huku akimtazama raisi wa DR Congo.

“Ima nana muna hitaji kuleta majeshi yenu nchini kwangu?”

“Ndio”

“Ila hapa nchini kwangu kuna vikosi vya Umoja wa mataifa ambavyo vina shirikiana na vikosi vya nchi yangu katika kuendelea kulinda amani?”

“Vina linda amani gani ikiwa wanajeshi wangu wame uwawa katika ardhi yako. Sasa hii ni vita yetu, sasa hivi ni wakati wa kuchukua usukati katika hili kwa maana walio letwa wana linda ila sisi tuna kwenda kupigana na kuvuruga ngome zao. Hatuwezi kuwachekea na damu za wapiganaji wetu ziende kwenda bure”

Raisi wa DR Congo akaka kimya kwa muda huku akionekana kutafakari aliyo ambiwa na makamu wetu wa raisi.

“Kwa sasa nchiyangu ina pitia mambo mengi sana. Nchi yangu endapo ita kubali kukaribisha vikosi vyako kuja kupambana namaadui nina imani kutakuwa na muingiliano kati ya vikosi vya kulinda ulinzi vya umoja wa mataifa, umoja wa Afrika na nchi yangu. Bado tuna pata uzito kukubaliana na ombi hilo”

“Muheshimiwa raisi samahani kama nita kuwa nina kuvunjia heshima. Ila ukweli ni kwamba ni lazima nchi yangu ilipize kisasi kwa hao wanao jiita Yakutumba pamoja na hao waasi wa Burundi wa FLN(National Liberation Front). ”

“Jambo la kuongozea”

Nilizungumza na watu wote wakanitazama.

“Hakuna ajuae uchungu wa mtoto zaidi ya mzazi. Sisi ndio tuna juauchungu wa wanajeshi wetu walio kufana hususani mimi nina tambua uchungu wa ambushi kwa wanajeshi. So muheshimiwa raisi tuingie mkataba wa wanajeshi wetu kuja nchini kwako na kuendesha oparesheni ya kuwaondo hao waasi”

Nilizungumza huku nikimtazama raisi wa DRC.

“Wewe ni nani?”

Raisi wa DRC aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.

“Mshauri wa makamu wa raisi”

“Basi kama nimshauri una paswa kukaa kimya na kumshauri kiongozi wako kimya na sio kutoa shinikizo la wazi wazi na unavyo fanya nikama vile una nilazimisha kufwata kile munacho kihitaji nyinyi ikiwa hii nchi ni yangu na maadui ni wangu.”

Raisi wa DRC alizungumza kwaa hasia kidogo na msisitizo. Makamu wa raisi akanipa ishara ya kukaa kimya na nisimjibu chochoye raisi huyu.

“Muheshimiwa raisi tuna hitaji jibu”

Makamu wa raisi akaongelea msumari wa moto ambao kidogo ukamfanya raisi wa DRC kushusha pumzi. Nikamtazama kwa umakini sana na kugundua kitu kwa raisi huyu.

”Nina kuheshimu sana makamu wa raisi, ila munacho kihitaji hamuto weza kukipata kwenye nchi yangu. Sinto kubali maeshi yenyu yaweze kuingia nchini kwangu. Kama muna jengine muna weza kuzungumza ila kama ni hilo nina omba mazungumzo haya yaishie hapa”

Mimi na makamu wa raisi tukatazamana kwa mshangao.

“Ni kitu gani unacho kificha muheshimiwa raisi katika waasi hawa?”

“Sifichi kitu, ila mamjeshi ya Marekani yalikwepo hapa miaka ya nyuma. Wakadai kwamba wata tusaidia kupanda na waasi hao, mwisho wa siku wakawa wana iba dhahabu zetu na kupeleka kwao hadi tumekuja kugundua hilo nchi ime kwisha kabisa”

“Unamfananishaje mfiwa na mkusanya rambirambi. Mkusanya rambirambi yeye hana uchugu na anacho kitazama ni maslahi ya rambirambi inayo patikana. Sisi tume fiwa na wanajeshi wetu, ndio maana tukio limetokea jana leo tupo hapa”

“Sina imani na nchi yoyote katika kuleta vikosi vyake ndani ya nchi yangu. Hivyo basi samahani sana muheshimiwa makamu wa raisi maamuzi yangu yame fikia hapo. Walizi wangu wata kulinda na kukurudisha uwanja wa ndege na uta rudi nchini Tanzania salama salmini.”

“Muheshimiwa raisi, babda nizungumze kwa niamba ya makamu wangu hapa wa raisi na nchi yangu. Utake na usitake, vikosi vyetu vitaingia nchini mwako, iwe ni kwa njia ya anga au ardhini ni lazima tumpige yule aliye tupiga. Sisi sio nchi nyingine ambazo ume wahi kukumbana nazo wakipata tukio kama hili la wanajeshi wao kuuwawa na wana rudisha miili yao katika nchi zao na kwenda kuzikwa. Huto jua muda, saa, au siku ambayo vikosi vyetu vita ingia kwenye nchi yakona mark my words. Mimi ndio nita viongoza vikosi hivyo kulipiza kisasi na hapo ndipo uta kuwa ni mwanzo mpya wa kuanzisha kikosi kingine cha X ambacho kikosi cha kwanza mimi ndio nilikuwa kiongozi wao, wakafa ila hichi cha sasa hivi nikuhakikishie kwamba hakuna ambaye ata kufa na usitarajie tuta kuja wengi ila tuta kuja wachache na tuta wachapa waasi hao na kama uta kuwa una shirikiana na baadhi ya waasi na tukafahamu, nina apa kwa jina la mama yangu aliye nitupa mtaroni jiandae kuachia madaraka yako kwa maana tutakutoa iwe ni kwa nguvu au hiyari. Mkuu tuondoke”

Mara baada ya kuzungumza maneno hayo nikanyanyuka na kuliweka koti la suti yangu vizuri na kumfanya raisi wa DRC na washauri wake kutokwa na macho ya mshangao kwa maana nina imani sifa za kikosi cha X walisha wahi kuzisikia miaka ya nyuma.



“Ngoja kwanza”

Raisi wa DR Congo alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.

“Una taka kuniambia wewe ndio ulikuwa kiongozi wa kikosi cha X?”

“Hilo ni jibu na sio swali”

“Ila nilisikia X wote walisha kufa?”

“Mzee una toka nje ya mstari. Mazungumzo yetu sisi na wewe yamekwisha, muheshimiwa tuondoke”

Makamu wa raisi akashusha pumzi huku akinitazama usoni mwangu na ninacho kizungumza nina maanisha.

“Kwa nini ume kataa tuyamalize haya mambo katika mazungumzo ya kawaida, hadi una lazimisha tufikie huku?”

Makamu wa raisi alimuuliza raisi wa DR Congo.

“Simuamini mtu yoyote sasa hivi. Nchi yangu ni nchi huru na ni nchi ambayo haipo mikononi mwa mtu yoyote, hatutawaliwi na mtu yoyote na hatupangiwi na mtu yoyote. Tuna ilinda mipaka yetu sisi wenyewe na hatuto hitaji msaada wa nchi yoyote ile duniani. Tuna shukuru kwa kuweza kuhudumu nasi kwa siku zote hizo na poleni kwa wanajeshi wenu kuweza kuwawa. Ila yote katika yote tuta endelea kuwa na mahusiano ya nchi kama nchi ila sio mahusiano ya kuisalama. Asanteni kwa kuja, walinzi wetu watawapeleka hadi uwanja wa ndege”

“Wewe huendi?”

Niliuliza huku nikimtazama usoni mwake.

“Nina kikao na katibu mkuu wa umoja wa mataifa hivyo sinto kwenda uwanja wa ndege kwa sasa”

“Sawa”

Raisi wa DRC akasimama pamoja na watu wake, huku makamu wa raisi naye akasimama pamoja washauri wake, huku mimi nikiwa ndio wa kwanza kusimama kabla ya wao.

“Nina ombi moja muheshimiwa raisi”

Makamu wa raisi alizungumza huku akimtazama raisi huyu.

“Hakuna shaka una weza kuomba”

“Nina omba niweze kuwatembelea wanajeshi wangu ambao wame jeruhiwa na walio salimika katika kambi iliyo vamiwa?”

Nikamtazama makamu wa raisi kwa macho ya mshangao.

“Ahaa muheshimiwa, hilo eneo ambalo una omba kwenda ni hatarishi kwa usalama wako na mimi sipo tayari kuwaweka rehani walinzi wangu kwenye eneo kama hilo. Ila kama vijana wako wata weza kukulinda, basi tuta wapatia escort ya polisi wacheche hadi karibu na eneo hilo na huko mbele ya safari muta kwenda nyinyi wenyewe”

Kauli ya raisi wa DRC kidogo ika nipa mashaka makubwa sana, nikamsogee makamu wa raisi na kumnong’oneza sikioni mwake.

‘Mkuu hilo eneo nikiwa kama mlinzi mwenye mamlaka kukuweka hai, nina kushauri usiende’

‘Ni lazima kwenda nikawatie nguvu wapigania amani wetu. Wamepoteza wezao na wata farijika kuniona kiongozi wao nime fika eneo lile. Tuna wanajeshi zaidi ya elfu moja na mia sita wapo katika nchi hii, hivyo ni jambo la muhimu mimi kufika katika eneo hilo. Kumbuka mimi ni mwanajeshi pia hivyo usiwe na mashaka katika dhiara hii. Upo na chuma cha pua”

Makamu wa raisi alinijibu kwa kuninong’oneza na kunifanya nimtazame usoni mwake na nika gundua anacho kizungumza ana maanisha.

‘Andaa timu yako’

“Sawa nime kubaliana nahilo na nita omba vijana wangu waweze kupatia nafasi ya kupanga mipango yao juu ya safari hiyo ya gafla”

“Hakuna shaka juu ya hilo na pia mukihitaji silaha na vitu vingine tuta julishana”

“Asante sana muheshimiwa raisi”

Makamu wa raisi alijibu kwa busara zote. Akili yangu sasa ikaanza kufanya kazi kwa kasi sana huku nikipanga mipango ambayo ita tufanikisha kuweza kuelekea katika eneo hilo hatari ambapo vikosi vya umoja wa mataifa, pamoja na wanajeshi wetu wana linda amani na usiku wa kuamkia leo wame toka kushambuliwa na kuuwawa.

‘Huyu mzee mbona ana taka kututoa sadaka?’

Nilijisema kimoyo moyo huku nikijaribu kutathimini umbali wa eneo ambalo tuna elekea na misitu ambayo tuta pita.

‘Mame walai”

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikitoka nje ya ukumbi huu wa mikutano. Judy akanifwata mara baada ya kuniona.

“Vipi mkuu mambo yamekwisha?”

“Safari ime badilika tuna hitajika kuelekea katika eneo ambalo wanajeshi wame uwawa. Makamu wa raisi ana hitaji kwenda kuona wanajeshi walio jeruhiwa na walio bakia salama”

“Mungu wangu, huko si hatari?”

“Ndio hivyo hapa ina bidi walinzi wote tuwe na kikao cha dharura”

“Je tuna kwenda na walinzi wa raisi wa hapa Congo?”

“Hapana, tuna pewa askari polisi na sio kwamba wana tupeleka hadi huko kwenye misitu, watatuacha mbali kidogo kisha safari ya kwenda huko ita kuwa juu yetu”

“Mmmm!!”

Judy aliguna huku akionekana kujawa na mshangao.

“Ndio hivyo idadi yetu tupo thelathini na mbili. Ila ngoja niwasiliane na ikulu ya Tanzania, makamu wa raisi akifa hapa mimi ndio nita hojiwa na sihitaji upuuzi”

“Kweli fanya hivyo mkuu”

Nikatoa simu yangu ambayo ina uwezo wa kupiga simu nikiwa nchi yoyote ile na ndio simu niliyo pewa na Maria na simu hii mazungumzo yake ninayo yafanya hayawezi kunaswa na mtandao wowote wa simu wala satelaite. Nikatafuta eneo ambalo lipo tulivu, nikampiga moja kwa moja katika ofisi ya raisi.

“Ikulu ofisi ya raisi nchini Tanzania. Una zungumza na Maria nani mwenzangu”

“Ni mimi, niunganishe na raisi sasa hivi”

“Eddy ni wewe?”

“Maria fanya hivyo nina haraka”

“Sawa”

Baada ya sekunde thelathini nikaisikia sauti ya raisi.

“Muheshimiwa ni mimi”

“Ndio X”

“Kikao hakijafanikiwa kama tulivyo kuwa tume kusudia. Hivi sasa makamu wa raisi ame panga tuelekee kwenye kambi ya wanajeshi wetu ambao ni jana tu wame vamiwa. Sasa muheshimiwa raisi mimi sija kubaliana na hili jambo kwa maana sehemu tunayo kwenda ni hatari na ni sehemu ambayo hatuto kuwa na ulinzi wa wanajeshi wa hapa Congo, yaani tuta kuwa sisi kama sisi. Asilimia sabini ya walinzi wa makamu wa raisi hawana uzoefu na mapigano ya misituni. Ita kuwaje hapo muheshimiwa?”

“Ni sawa, nilisha liongea hilo jambo na makamu wa raisi kwa yeye kwenda kuwatembelea wanajeshi wetu. Na tumesha zungumza na mkuu wa vikosi hivyo na wata wapokea katika hilo pori hivyo musiwe na shaka kwa maana kuna maagizo nime mpa akawapatie wanajeshi wetu”

“Sawa”

Nikakata simu huku nikishusha pumzi nyingi kwa maana nilicho kuwa nina kitarajia kukisikia kwa raisi sio hichi alicho nijibu. Nikarudi eneo alipo simama Judy.

“Wamesemaje?”

“Raisi ana fahamu juu ya hili jambo la kwenda huko”

“Fuc**”

“Yaa so niandalie kikao cha dharura na walinzi wote sasa hivi. Nina kuja kuzungumza nao”

“Sasa tuna kutania wapi?”

“Njee siamini hii ikulu. Kwenye vyumba vyao wana weza kufunga vinasa sauti ikala kwetu kila tutakacho kipanga basi wata kisikia.”

“Nime kuelewa mkuu”

Nikarudi ndani ya ukumbi na kumkuta makamu wa raisi na raisi wa DR Congo wakicheka kwa furaha sana.

“Muheshimiwa raisi nita omba kupatiwa ramani ya kuelekea huko na pia nita omba kupatia gari sita zenye ubora na ulinzi mzuri”

“Hilo halina shaka kijana. Hizo V8 zote haziinigii risasi, hivyo tuta kupatia gari unazo zihitaji. Je muna silaha za kutosha?”

“Ndio”

“Sawa ni jambo jema. Mkuu wangu huyu wa jeshi ata kwenda kukupatia hiyo ramani na maelekezo machache juu ya eneo munalo kwenda.”

“Nashukuru”

Nikaongozana na mkuu huyu wa jeshi hadi kwenye moja ya ofisi. Akanipatia ramani kubwa na kuiweka mezani.

“Kijana sija penda jinsi ulivyo kuwa una zungumza na raisi wangu. Musijione nchi yenu ina nguvu ya kipesa na kijeshi basi muone kwamba muna weza kumpangia kila mtu malaka ya kufanya kile munacho taka nyinyi. Tume elewana?”

“Sijakuelewa na sinto kuelewa. Laiti kama kungekuwa na mwanao emeuwawa huko Semulika, unge kaa na kitambi chako na kuniambia porojo kama hizo unazo zungumza sasa hivi. Nipe ramani, nipe maelekezo yaliyo sahihi, kisha swala hili muta dilia na mimi mara baada ya kumrudisha makamu wangu wa raisi nyumbani”

“Una juamini nini wewe kijana?”

“Najiamini kwa maana mimi ni shetani. Hivyo mzee, musije mukajaribu kunichoma kisu kwa nyuma kwa maana, hata Mungu hajui ni nini nita kifanya”

Nilizungumza kwa kujiamini huku nikimtazama mzee huyu aliye valia nguo zake za kujeshi zilizo jaa vyeo vingi. Tukatazamana kwa dakika tano kisha akatingisha kichwa huku akitabasamu, akaanza kunipa maelekezo ya wapi na wapi tuna paswa kwenda na kupita. Nilipo ridhika nika ikunja ramani hiyo kabla ya kutoka nje ya ofisi hii akaongea neno la lugja ya ki Potrgues ambacho nina kielewa. Maana ya neno hilo alisema hii ni DR Congo. Nikamgeukia na kumjibu kwa luga hiyo hiyo.

“Sisi ni Watanzania, na usidhubutu kujichanganya na sisi, tuta wafanya zaidi ya kile alicho fanywa IDDI AMIN, Uganda”

Mara baada ya kumzungumza hivyo, mzee huyu macho yakamtoka kwa mshangao kwa maana alihisi kama sifahamu lugha yake. Nikafungua mlango na kutoka ndani hapa, nikaongozana na Judy hadi sehemu walipo walinzi wote kutoka nchini Tanzania. Walio kosekana hapa ni John, Maulid na mlinzi wengine ambao kazi yao ni kuwa na makamu wa raisi muda wote kwa maana hatumuamini mlinzi yoyote wa hapa DR Congo kwani wana weza kutuchezea mchezo mchafu na mambo yakaenda ndivyo sivyo.

“Nina imani mume weza kusikia kwamba haturudi Tanzania leo. Tuna elekea Semuliki eneo la Beni katika mkoa wa Kivu Kaskazini. Wote muna jua ni kitu gani kilicho tokea katika eneo hilo, sina haja ya kuadithiana. Kila mmoja atambua kwamba tuna kwenda katika sehemua ambayo ni hatari sana. Akili mawazo yetu sasa hivi yasifikirie nyumbani Tanzania. Yafikirie kwa nini tupo hapa na sisi sote nina hitaji tuweze kurudi tukiwa hai nchini mwetu. Tume somana?”

Nilizungumza kwa msisitizo huku nikiwakazia macho.

“Ndio mkuu”

“Nina swali mkuu”

“Uliza”

“Tuna kwenda kufanya nini?”

“Okay nilisahau. Makamu wa raisi anahitaji kwenda kukutana na wanajeshi wetu wa Tanzania. Hayo mengine yanayo kwenda kuzungumza huko, mimi sifahamu. Kitu kingine ni kwamba, tuna pewa askari polisi kutusindikiza”

Walinzi hawa wakatazamana.

“Jambo jengine ni kwamba hii safari ni ya masaa zaidi ya arobaini”

“Mungu wangu!!?”

Judy alihamaki.

“Mkuu ni sawa kweli, siku mbili tukazimaliza tukiwa barabarani ikiwa kuna usafiri wa ndege?”

Mlinzi mwengine aliuliza.

“Ni kweli mkuu, hiyo Kivu ipo karibu na Uganda huko, huoni ni hatari kwa usalama wetu na makamu wa raisi. Hembu tuna omba uka zungumze naye. Tupewe hata helicopter zitupeleke huko, tuokoe muda”

Walinzi walinishauri na sikuhitaji kukataa mawazo yao nikarudi kwenye ukumbi na kumnong’oneza makamu wa raisi juu ya maoni hayo ya walinzi wake.

“Siamini usafiri wa helicopter hususani kwa nchi kama hii, endapo helicopter ikishambuliwa, nini muta fanya, wote tulipukie hewani. Nimesha jianda akwa hili na nina jua ita chukua siku mbili wewe nenda kawaambie wawe tayari kwa safari hiyo”

Makamu wa raisi alinijibu kwa kuninong’oneza sikioni mwanangu.

“Sawa”

Nikarudisha jibu kwa walinzi na kila mmoja akaonekana kukubali kishingo upande kwa maana sisi sote hakuna mwenye mamlaka ya kumzidi makamu wa raisi na akitoa agizo kazi yetu ni kufwata tu.

“Kila mmoja simu yake iwe online. Ramani ya kutoka hapa kuelekea huko, kila mmoja ita soma kwenye simu yake sasa hivi, nime tumiwa kutoka ikulu ya Tanzania. Gari tutakazo zitumia ni zile za jana, gari tumesha andaliwa na tukumbuke tuta panda fery mara tatu na kila kivuko kimoja cha Ferry tutatumia dakika ishirini. Hivyo let’s go”

Walinzi wakatawanyika huku wengine wakikagua magari ambayo tumesha andaliwa.

“Mkuu samahani kwa kutumia neno hili, ila huu ni uchizi una endelea. Masaa aruboini na ushee tutumie barabarani. Sio jambo zuri kwa kweli”

Judy alilalama huku uso wake ukilengwa lengwa na mchozi. Nikasimama na kumtazama machoni mwake.

“Judy”

“Ndio mkuu”

“Kama Mungu amepanga turudi salama basi tuta rudi salama ila kama ame panga tufie hapa basi miili yetu ita rudishwa Tanzania kwa heshima kubwa. Hivyo usiwaze mdogo wangu kika kitu kita kwenda salama”

“Sawa mkuu”

“Usiogope uta kwenda kumuona boyfriend wako tena”

Judy akatabasamu, nikaingia kwenye ukumbi na kumnong’oneza makamu wa raisi kwamba maandalizi yote yapo vizuri. Wakaagana na raisi wa DR Congo kisha tukatoka nje na kuingia kwenye magari haya humu, mimi, Maulid, Judy na makamu wa raisi tukipanda kwenye gari moja na walinzi wengine wakipanda magari mengine. Wakati huu Maulid ndio dereva wa gar hili la tatu kutokea nyuma. Nikatazama bendera ndogo za Tanzania zilizo fungwa kwenye magari haya yote.

“Watu wote mupo tayari?”

Nilizungumza kwa kutumia kinasa sauti changu, na kila mlinzi alijibu kwa kunitajia code namba yake, na zilipo fika thelathini na moja huku mimi nikiwa wa thelathini na mbili, nikaruhusu msafara huu kuanza safari ya kuondoka eneo hili. Gari nne za polisi wa hapa DRC, mbili zikatangulia mbele yetu kutuongoza njia huku mbili zikiwa nyuma ya gari zetu za msafara huu. Ukimya ukatawala ndani ya gari letu huku kila mmoja akionekana kujawa na mawazo yake.

“Mkuheshimiwa?”

“Ndio”

“Kwa nini tuna tumia muda mrefu sana kwenye hii safari?”

Swali la Judy ambaye dhairi anaonekana kuto ridhishwa na safari hii aliuliza.

“Nahitaji kuifahamu DRC vizuri”

“Kuijua tu?”

Maulid aliuliza kwa mshangao.

“Ndio”

Judy na Maulid wakajawa na mshangao, nikamtazama makamu wa raisi, mzee ambaye nilikaa naye kwa muda mrefu sana nika fanikiwa kujua kuna kitu kinacho endelea juu ya safari hii ambacho sio rahisi kwa walinzi wa kawaida kuweza kufahamu.

“Mkuu ni kitu gani kina endelea?”

Ilibidi nimuulize makamu wa raisi mimi mwenyewe huku nikiwa nime zima kinasa sauti changu ili mazungumzo yetu yasiweze kusikiwa na mtu yoyote.

“Katika upelelezi wangu nilio kwa kuzungumza na wale viogozi, ina onyesha kwa asilimia kadhaa kwamba serikali ina husika katika hili shambulizi. Hivyo katika huu msafara wa kuelekea huko, kuna asilimia kubwa ya kumjua adui yetu ni nani”

“Okay hapo nina anza kupata picha”

“Yaa. So raisi na viongozi wake wa ngazi za juu ni lazima wata tafuta mbinu nanamna gani ambavyo wana weza kutimaliza tukiwa ndani ya hii ardhi yao na endapo wata fanya hivyo basi, nchi kama nchi yetu haito kuwa na excuse yoyote katika kufanya mashambulizi, ambayo yata wajumlisha wanajeshi wa serilali na waasi”

“So una taka kuniambia tuna taka kuitawala DRC?”

“Hapana hatitawali ila sisi kama nchi yenye nguvu Africa na duniani, lazima tuwe na uwezo wa kupanga nani ana tawala sehemu fulani na nani ana paswa kuondoka sehemu fulani kwa muda tunao ona sisi una faa. Kikubwa ni kuhakikisha tuna weka viongozi ambao wata kuwa chini yetu na tuta pata maslahi kwa kuweka viongozi hao madarakani. Hivi ndivyo alivyo kuwa ana fanya Marekani kwa miaka ya nyuma ndio maana utajiri wa Marekeni ulikuwa ni mkubwa hadi sisi tulivyo weza kufanikiwa kupata hadhina ya dhahabu iliyo vumbuliwa na kina Julieth na Magreth viongozi wetu wa nyuma na kutupelekea kuwa nchi yenye nguvu na tajiri duniani kwa sasa”

Nikamtazama makamu wa raisi usoni mwake kisha nikatabasamu kwa maana huu ni mtego na endapo viongozi hawa wa DRC wakijichanganya na kutushambulia katika safari yetu basi ndipo unapo kuja ule usemo wa nikanyage bahati mbaya nikupige makusudi.



Gari zote zina tembea kwa spidi moja moja na stidi, spidi ambayo kwa gari kama hizi V8 ni kubwa sana kwani injini zake zina nguvu isiyo ya kwaida. Jambo la kumshukuru Mungu ni kwamba kila eneo ambalo tulikuwa tuna pita magari yaliweza kusimamishwa. Tukaumaliza mji wa Kinsasha salama Salmin na safari ikazidi kusonga mbele, msafara wetu haukusimama hata pale giza lilipo tawala anga. Nikatazama saa yangu ya mkononi na kukuta ni saa nane usiku.

“Madereva wabadilishwe”

Niliwaambia walinzi wote kwenye gari zote kwa maana nina tambua wata kuwa wamechoka kwani tumesha maliza zaidi ya kilomita elfu moja na sasa tume bakisha kilomita elfu moja mia saba na kumi na moja. Tukafika Tshilenge District, msafara ukasimama na madereva wakapokezana huku kwa wakati huu akiendesha Judy kwenye gari hili tulilo panda na safari ikaandelea huku gari za askari zikidizi kutuongoza.

“Nimekaa hadi mgongo una niuma”

Makamu wa raisi alizungumza huku akijinyosha nyoosha.

“Ndio hivyo muheshimiwa safari bado ni ndefu sana. Maulidi vipi upo poa?”

“Ndio mkuu nipo fresh”

“Una dakika thelathini za kulala”

“Nashukuru mkuu”

Tartaibu Maulida akaikunjua siti aliyo kaa na kulala, kwani hata Judy naye nilimpa muda wakutosha kwa ajili ya kulala.

Majira ya saa kumi na moja alfajiri tukafanaikiwa kuingia katika Lomani.

“X”

“Ndio muheshimiwa?”

“Ina bidi vijana sasa wapumzike”

“Tume bakisha muda machache kufika katika mji wa Kabinda, ngoja nijaribu ku google hoteli zilizopo katika eneo hilo”

Nikatoa simu yangu mfukoni na kuingia kwenye mtandao na kutafuta hoteli ya haraka haraka na nikwafanikiwa kupata hoteli iitwayo Ka-be de Luxe. Nikakagua huduma zote zinazo patika katika hoteli hii, pia nika kagua maeneo ya hoteli hiyo kwa kutumia satelaite. Nilipo jiridhisha nikawasiliana na meneja wa hoteli hiyo na kumtaarifu ndani ya dakika kumi na tano tuta kuwa katika hoteli yake.

“Ume sema ni mlinzi wa makamu wa raisi wa Tanzania?”

“Ndio, mbona una maswali mengi?”

“Okay nime elewa”

“Sawa”

Nikawataarifu walinzi wote juu ya kufika hotelini hapo kwa ajili ya kupata chakula na safari yetu ita endelea kwa maana hata kama ni wakakamavu vipi ila unapo kuwa na njaa basi kila kitu kina weza kwenda vibaya. Ndani ya dakika kumi na tano kama nilivyo muahidi meneja wa hoteli hiyo, tukafika hotelini kwake.

Walinzi kadhaa wakashuka kwenye magari na kuingia katika hoteli hiyo na kuikagua kwa dakika kumi, walipo jiridhisha tuka shuka kwenye gari huku tukiwa tume muweka makamu wa raisi katikati. Walinzi kadhaa wakaingia jikoni na kuandaa chakula kwa maana hatuhitaji kupikiwa na wapishi wa hoteli hii japo vyakola ni vyao. Marabaada ya ugali na mchicha kukamilika, tukala na kushiba vizuri, japo ni asubuhi. Mara baada ya kumaliza kula, tukawalipa kiasi wanacho tudai na safari ikaendelea huku wakati huu tukihakikisha kwamba tuna tumia masaa sita kufika katika mji tunao elekea.

“Ila nchi hii ina ufisadi mkubwa sana. Yaani ime barikiwa kila kitu ila ufisadi na uroho wa madaraka una warudisha nyuma”

Makamu wa raisi alizungumza huku tukitazama baadhi ya maeneo haya tunayo yapita jinsi yalivyo haribiwa kwa mashambulizi ya mabomu. Nyumba nyingi za wananchi zime chomwa moto, huku umasikini ukiwa ume kithiri sana kwao.

“Wana siasa muda mwengine wana sababisha hali za nchi zao kufika katika maeneo kama haya”

“Ni kweli, ila una jua demokrasia iliyopo Tanzania, Mungu ametubariki sana, ndio maana muda mwengine tuna kuwa wakali kwa washenzi ambao ana taka kuiingiza nchi kwenye machafuko”

“Hilo unalo lisema ni kweli mkuu. Sema kuna watu hawaijui vita ndio maana wakikaa kwenye nchi kama Tanzania basi wana jaribu kuleta chokochoko za hapa na pale. Sasa watu kama wale ukiwaleta hapa Congo hawato tamani kumaliza siku hata moja”

“Yaa. Ila katika utawala wetu, mtu akileta upumbavu, ndani, tukiona bado haja jielewa ana potea hewani. Hatuwezi kuziweka rehani roho na mamilioni ya Watanzania kisa mpumbavu mmoja au wapumbavu kadhaa na chama chao”

Makamu wa raisi alizungumza kwa msisitizo.

“Ni kweli kwa manaa hakuna mwenye nguvu kuliko nchi.”

“Alafu muda mwengine huwa nina shindwa kuelewa wale wana siasa wana toka vyuoni na kusoma maswala mengine na hawajui mifumo ya kiusalama, wanavyo kaa na kuropoka, ohoo nchi haina hili wala hili, sijui kimepanda kime shuka na X uta niambia. Hili tukio wata litumia kama kigezo cha kumshinikiza raisi kuwarudisha wanajeshi wetu nyumbani na wasiendelee kulinda amani kwenye nchi zisizo na amani kama hizi”

“Sasa mkuu endapo wata washinikiza ni nini mutakacho fanya?”

“Mimi sema ni makamu wa raisi, ile ninge kuwa ndio raisi. Haki ya Mungu nina kuambia, mtu akifungua kinywa chake na kuleta ujinga kisa wanajeshi wetu walio uwawa. Nina mkamata, yeye na watoto wake wa kiume alafu tuna wapeleka jeshini. Wakipata msoto wa miezi sita, wakirudi wata kuwa na akili”

“Hahaaa”

Sote ndani ya gari hili tukacheka.

“Haki ya Mungu nina waambia. Yaani nina wapelekea kwenye kila kitengo cha mizinga kule, wakiona jinsi watu wanavyo randuka kwa kufyatua mizinga, nao akili zao zita randuka. Yaani nina wachukia sana wana siasa midomo ambao wana fikiria matumbo yao kuliko kufikiria amani ambayo tulitengenezewa na wazee wetu kwa miaka mingi iliyo pita. Alafu kwa nini X ukifikisha miaka kama arobaini na tano hivi usiingie kwenye siasa”

“Duuu mkuu kwenye vitu ambavyo sikuwahi kuviwazia ni kuingia kwenye siasa?”

“Kwa nini, una jua tukianza kukusuka na kuwa kiongozi sasa hivi, nina imani hapo baadae Tanzania ita pata kiongozi mahiri na hodari, sisi wezako umri ndio una kwenda, miaka ya kuishi nayo ina kwisha.”

“Anacho kizungumza muheshimiwa ni kweli, mkuu kwa nini usiingie kwenye siasa?”

Judy naye alimuunga mkono makamu wa raisi.

“Hapana jamani, mimi siwezi siasa”

“Kwani mimi nilikuwa nina iweza X. Wewe mwenyewe una jua nilikuwa jeshini na nimelitumikia jeshi kwa miaka arobaini na mbili. Ila nilipo ona kuna nafasi ya mimi kuingia kwenye siasa nika itumia na leo nime fanikiwa”

“Duuu sijui kwa kweli kama siasa nita iweza”

Taratibu magari yakaanza kupunguza mwendo na kusimama.

“Kuna nini kinacho endelea?”

Nilizungumza huku nikiwauliza walinzi walipo gari la mbele.

“Mkuu naona askari mwisho wao ume ishia hapa. Tuna ingia South Kivu”

Nikafungua mlango wa gari hili na kushuka, huku kwenye kila gari moja akishuka mlinzi mmoja. Nikamfwata mkuu wa polisi ambaye ameongozana nasi katika safari hii.

“Tuna watakia safari njema ndugu zetu”

“Tuna shukuru sana”

Nikapeana mkono na mkuu huyu wa polisi, kisha wao wakageuza gari zao na kuanza safari ya kurudi tulipo toka. Nikashusha pumzi huku nikitazama kibao kilicho andikwa kwa kifaransa, Karibu Kivu, nikatoa ishara ya walinzi wote kurudi ndani ya magari, huku nami nikiingia kwenye gari ambalo yupo makamu wa raisi.

“Haya sasa tupo sisi kama sisi, umakini una hitajika na tuna paswa kutembea kwa mwendo wa umakini, plate namba za gari zote zitolewe na vibendera vya Tanzania zote zitolewe”

Nilitoa maagizo hao na yakatekelezwa kwa uharaka huku Maulid kwenye gari letu yeye ndio ana fungua plate namba pamoja na kuitoa bendera ndogo iliyo kuwa ina pepea mbele ya gari letu.

Baada ya zoezi hili kuisha safari ikaanza tena upya huku tukiwa na masaa kumi na nne kuitafuta North Kevu, huku.

“Jamani huu ni mji hatari na tuna kiviko kimoja cha Fery kilicho salia ina tupasa kuendelea kuwa macho kwa kila muda na tuna kilomita 522”

Nikaitazama saa yangu ya mkononi ina onyesha sasa hivi ni majira ya saa saba mchana. Tukazidi kupita mabonde ma milima, hadi tukaifka kwenye kivuko, cha Fery majira ya saa nne usiku, safari ikaendelea na tukafanikiwa kufika Goma katika mtaa wa Mailitatu majira ya saa nane usiku. Saa kumi na moja alfajiri, tukafika Mabenga. Nikaamrisha msafara kusimama kwa maana tunapo ingia sasa tupo kwenye zone ya maadui, kwani sasa tumesha ikanyaga North Kivu. Nikawasiliana na wanajeshi ambao tume ambiawa wata tupokea.

“Nina itwa X, ni kiongozi wa msafara wa makamu wa raisi”

“Ohoo tume pewa habari zako, sasa hivi tupo katika mji wa Rwindi, tuna weza kukutania hapa?”

“Bila shaka je hali ya usalama ipo vipi?”

“Sio shwari kwa maana bado tuna pambana na adui aliye vamia kambi yetu hivyo muna ingia kwenye zone ya vita”

“Sawa nime kuelewa Captaine.”

Nikakata simu na safari ikazidi kusonga mbele huku tukianza kukatiza kwenye misitu mineno na iliyo shone kisawa sawa. Mbaya zaidi barabara hii ni ya vumbi na ina mabonde bonde yanao fanya magari yasiende kwa mwendo wa kasi. Nikaitoa bastola yangu kabisa na kuishika mkono wangu wa kushoto huku macho yangu kiwa makini sana kutazama msitu huu. Tukaanza kusikia milipuko ya mabomu iliyo wafanya maderava wa gari za mbele kusimamisha magari.

“Mkuu huku tunapo kwenda kuna milipuko ina kuwaje?”

Dereva wa gari la mbele aliniambia, nika shusha pumzi huku nikisikilizia ni wapi milipuko hiyo inapo tokea, kwa ujuzi wangu, nika gundua milipuko hiyo haipo mbali sana kutoka hapa tulipo. Nikatoa simu yangu na kumpigia Capten.

“Ndio X”

Alizungumza kwa sauti kubwa huku nikisikia milio ya risasi.

“Mupo wapi?”

“Hili eneo tulilo kuwa tuna wasubiria tume vamiwa na adui hivyo tuna pambana na nina washauri murudi mulipo toka”

Ikabidhi niiweke simu yangu loud speaker ili makamu wa raisi aweze kusikia kinacho endelea.

“Mume vamiwa?”

“Ndio na wanajeshi kadhaa wameuwawa. Rudini tuu”

Nikamtazama makamu wa raisi usoni mwake.

“Ina bidi twende”

Makamu wa raisi alizungumza na sisi wote macho yakatutoka.

“Seriously?”

Nilimuuliza makamu wa raisi huku nikimkazia macho.

“Ndio ina bidi twende”

“Bila ya kukuvunjia heshima mkuu. Siwezi kuwatoa sadaka walinzi thelathini na kwa ajili ya kuigia eneo ambalo wanajeshi wenye silaha na uwezo wa kupigana msituni wakafaa. Nina malka na majukumu ya kukuruidisha salama nchini Tanzania. So tuna rudi Goma, tunarudi Tanzania. Maamuzi yangu yameishia hapo”

Nilizungumza kwa msisitizo huku nikimtazama makamu wa raisi usoni mwake.

“X hatuwezi kula ng’ombe mzima tuka bakisha mkia. Ina bidi tufike kwenye hiyo kambi”

“Najua hamu na hamasa yako ya kuwaona wanajeshi wako. Utafanya dhiara wakati mwengine ila kwa sasa sihitaji watu wangu kuingia kwenye shida inayo epukika muheshimiwa”

Ilibidi nifoke kwa maana nikimuendekeza mzee huyu tuna weza kufa kwa ajili ya upumbavu ikiwa walinzi wengi umri wetu ni miaka thelathini na ushee, ila yeye emesha kula chumvi vya kutosha. Maulid na Judy wote macho yao yapo siti za nyuma wakitutazama mimi na makamu wa raisi.

“Hii ni amri na sio ombi. Tuna pita kwenye hilo eneo na kufika kambini. Judy washa gari tuendelee na safari”

Makamu wa raisi alizungumza kwa msisitizo huku akinikunjia sura. Judy na Maulid wakanitazama mimi usoni mwangu kwa maana wapo chini yangu. Nikashusha pumzi na kumpigia captain.

“Haloooo”

Captein alizungumza kwa sauti ya juu sana,kwani milio ya risasi na mabomu bado ime rindima

“Tuna kuja”

“Nini?”

“Nasema tuna kujaa sasa hivi”

Nilizungumza kwa hasira huku machozi ya hasira yakinilenga lenga usoni mwangu.

“Mume changanyikiwa, nimesema rudini mulipo toka, maadui zetu wana zidi kutushambulia muna yaweka maisha ya makamu wa raisi rehani”

Makamu wa raisi akanipokonya simu.

“Ni mimi makamu wa raisi wa jamuhuri ya Muungano wa Tanzania. Nina kuja eneo la vita”

“Muheshimiwa makamu wa raisi, tafadhali nina kuomba sana tena sana murudi tu. Hali ya usalama ina zidi kuzorota kila dakika”

“Hili sio ombi ni amri”

Makamu wa raisi mara baada ya kuzungumza maneno hayo akakata simu na kunikabidhi huku akinitazama usoni mwangu.

“Sijaongozana na watu waoga. Watu wasio jimudu, watu wanao ogopa vita. Nime ongozana na watu hodari, majasiri na wenye uwezo wa kumlinda kiongozi wao no matter what. So tuna kwenda, na sihitaji mtU kupinga amri yangu.”

Makamu wa raisi alizungumza huku akinikazia macho.

“Hili ndio ombi langu la mwisho kwenu nyote nikiwa kama kiongozi wenu. Kwa pamoja tumuombe Mungu kila mmoja kwa imani yake, tuweze kuingia pamoja na tuweze kutoka pamoja. Amen”

Mara baada ya kuzungumza maneno hayo, kila mmoja akatulia kwa dakika moja. Ilipo isha nikatoa ruhusa ya kuianza safari ya kuingia katika msitu ambapo mapigano kati ya wanajeshi wanao linda amani nchini DRC pamoja na waasi wa nchi DRC yana endelea na sisi ina tupasa kupita katikati ya eneo hilo ambapo sijui kama tuta fanikiwa.



Nikamtazama makamy wa raisi na wala sikuhitaji kumsemesha chochote. Kila jinsi gari zinavyo zidi kwenda divyo jinsi milio ya risasi na mabomu inavyo zidi kurindima. Baada ya mwendo wa dakika kumi na tano gafla dereva wa gari la mbele akasimamisha gari lake. “Mkuu kuna gari la jeshi lina teketea kwa moto na njia ime vibwa” Dereva wa mbele alizungumza na walinzi wote tuliweza kumsikia. “Hakuna njia kabisa?” “Ndio muheshimiwa hatuwezi kupita na njia ni moja” “Gari lina ukubwa gani?” “Ni lori muheshimiwa” Mvua nzito ikaanza kunyesha huku radi zikirindima.

‘Huu sasa uchawi?’

Nilijisemea kimoyo moyo kwa maana mvua hii ni mvua ya gafla sana na ina nyesha kwa kasi ya hali ya juu. “Muangalieni makamu wa raisi” Nilimuambia Judy na Maulidi, huku nikifungua mlango wa gari hili huku mkono wa kulia nikiwa nime shika bastola. Nikaanza kukimbia kwa kasi hadi lilipo gari la kwanza. Nikaona jinsi liri kubwa la jeshi jinsi linavyo teketea kwa mdua na inavyo oyesha lime fanyiwa shambulizi la bomu. Pembeni ya barabara hii kuna maporomoko ambayo endapo gari litadumbukia basi waliomo wote ndani wata kufa. Nikawapa ishara walinzi wa gari la mbele kwamba asishuke mtu. Nikapandisha kwenye gema lililopo pembeni ya barabara hii na kutazama upande wa pili wa barabara ambapo lori hili lime ficha sehemu hiyo.

“Ohoo Yesu wangu” Nilizungumza huku nikitingisha kichwa kwani kuna miili ya wanajeshi wapatao kumi ikiwa ime lala chini huku ikiwa ime uwawa kikatili sana. Nikavaa miwani yangu yenye uwezo wa kuweza kuona eneo hili lama kuna adui aliye jificha. Nikawaona wanajeshi ambao ni maadui wakiwa wamejibaza kwenye misitu upande ambao wanajeshi wameuwawa, huku wakionekana kusubiria sisi tupite.

“Nimee ona wanajeshi hamsini wenye bunduki pamoja na mabomu aina ya GPRS. Wana tusubiria sasa. Nahitaji gari zote ziweze kurudi nyuma na zifichwekwenye vichaka” Nilitoa agizo hilo huku nikishuka kwenye gema hili lililopo pembezoni mwa barabara. Nikimbia hadi kwenye gari letu na kuingia ndani. Magari ya yakarudi nyumba hadi kwenye eneo ambalo tuliona ni salama na gari zote tukazificha eneo hilo na kuacha barabara ikiwa wazi. “Maulidi” “Ndio mkuu” “Tuna kwenda sisi wawili nyinyi wengine mulio sahlia hakikisheni kwamba makamu wa raisi ana kuwa salama” “Mkuu muna kwenda wawili?” Judy aliniuliza kwa mshangao.

“Ndio” Nikazima kinasa sauti changu na kumtazama usoni mwake.

“Wewe ndio mtu wa pekee ninaye kuamini juu ya kumlinda makamu wa raisi hivyo kaa naye. Mkuu, nikifa uta muambia mke wangu nina mpenda sana ila nikirudi salama. Sinto hitaji kuifanya hii kazi hata kama utatakwa.” Mara baada ya kuzungumza hivyo nikashuka ndani ya gari na kufunga mlango kwa ndani. Nikafungua mlango wa nyuma kabisa ya gari hili na kutazama bunduki zilizipo eneo hili. “Mkuu una uhakika tuna washinda?” “Vita ni akili sio mabomu wala silaha” “Nimekuelewa mkuu” Nikachukua bundiki moja yenye uwezo wa kulenga masafa ya mbali, nikachukua mkanda wenye vifuko vya kuchomekea magazine. Nikauzungusa kiunoni mwangu na kuanza kuzichomeka magazine kumi na mbili za bunduki hii pamoja na magazine sita za bastola yangu na kila magazine ime jaa risasi. Maulida naye akajiandaa vizuri. Nikawasha kipaza sauti changu. “Wote mulio baki hakikisheni kwamba makamu wa raisi ana kuba salama na kama likitokea lolote rudini nyuma na muelekee Goma kuna uwanja wa ndege, na muta jua cha kufanya kuanzia hapa ili murudi nyumbani nchini Tanzania. Tumeelewana?” “Ndio mkuu” Nikakamtazama Maulid usoni mwake. “Vipi una ogopa?” “Hapana mkuu” “Kweli?” “Ndio siogopi” “Twende zetu” Tukaanza kukimbia msitu kwa msitu, tukafika kwenye kilima cha karibu kabisa na eneo walipo jificha maadui zetu. “Una waona?” Nilimuuliza Maulid huku tukiwa tume vaa miwani zetu. “Ndio” “Yule pale ndio kiongozi wao. Ambaye yeye ndio aliye anzisha vikosi hivi kwa ajili ya kupiaga na nchi yao. Tukimkamata yule hawa wote wata sarenda” “So mkuu tuna fanyaje?” “Tuna wavamia kutoka nyuma, moja wata amua kuruka kwenye korongo au wapande huku kwenye magema. Wewe baki hapa nahitaji unitungulia mmoja baada ya mmoja, nahitaji uwe the best sniper kwenye hili.” “Nimekupata mkuu” Maulidi akaifunga bunduki yake ya kiwambo cha kuzuia kelele. Nika zunguka eneo la nyuma walipo wanajeshi hawa wanao onekana kutusubiria kwahamu. Nilipo hakikisha kwamba nime kaa kwenye eneo ambalo nipo vizuri kwa kuwashambulia. Nikafunga kiwambo cha kuzuia sauti kisha nipiga goti moja chini huku bunduki hii ikiwa vizuri mkononi mwangu. “Maulid” “Ndio mkuu” “Niangushie mkuu wao mpige risasi mbili kwenye miguu yote mwilili, sasa” “Rogue than boss” Nikamshuhudia mkuu wao akianguka chini mzima mzima,jambo lililo wafanya wanajeshi wake waduwae huku wakijiuliza kime tokea nini. Nikaanza kuminina risasi kuelekea walipo, kila risasi niliyo ifyatua ina ina anguka na mtu na sehemu ambayo nina chagua kulenga ni shingoni au kichwani. Wapiganaji hao wanao ipinga serikali ya DRC wakazidi kuchanganyikiwa kwa maana hawajui risasi zina toka wapi na jambo hilo likawafanya wafyatue risasi hovyo hovyo. Idadi yao kila muda unavyo zidi kwenda ndivyo jinsi walivyo zidi kuanguka chini na kupungua. Nikazidi kulisogelea eneo lao huku kwa mara kadhaa nikihama maeneo ninayo shambulia.

“Dogo vipi?” “Your son of bitch boss.” Maulid alijikuta akitukana kwa furaha kwa maana hakuwa na imani kama tuna weza kuwamaliza wanajeshi hao ndani ya muda mfupi. “Niachie watato na mkuu wao” “Sawa boss” Maulid akapiga risasi wanajeshi watano kila mmoja kwenye mikono yake na na miguu na kuwafanya walale chini wakose msaada. Nikamaliza kuwaua askari watatu ambao walikuwa wamemzunguka bosi wao. Taratibu nikajitokea katika eneo ambalo tumewachinja kama kuku.

“Maulid nilide” “Eneo lipo safi boss hakuna anaye nyanyuka” Maulid alizungumza huku akiwa katika kilima nilicho muacha ambacho kina msaidia kuona eneo hili vizuri. Nikamsogelea mkuu wao anaye hema mithili ya joka kubwa lililo bananishwa. “Wewe ni nani?” Aliniuliza huku akinitazama kwa macho yaliyo jaa wekundu mithili ya mtu aliye vuta bangi. “X” Mkuu huyo macho yakamtoka kwa mshangao.

“Muna jifichaje eneo kama hili, mulihisi sisi ni kuku tunao kwenda kichwa kichwa?” “Tuongee dili, niache niondoke na sinto kanyaga tena DRC?” “Mimi sipo hapa kwa ajili ya kuiwakilisha DRC. Nipo hapa kwa ajili ya kuiwakilisha Tanzanaia. Ume tuulia wanajeshi wetu, una hisi nita kuacha salama?” Nilizungumza huku nikitoa simu yangu mfukoni, na kuanza kumrekodi mahojiano haya niayo yafanya na mkuu huyu wa waasi. Nikampiga picha kadhaa na kuzituma kwa walinzi wote nilio ambanana nao huku picha hizo nikizitupa pia ikulu nchini Tanzanua pamoja na video niliyo rekodi miili ya wanajeshi hawa waasi niliyo iua. “Vijana wako naona wana tokwa na damu nyingi hawapaswi kufa” Nilizungumza huku nikigeuzia simu yangu ninayo rekodi kwenye eneo walipo anguka vijana wake. Nikaanza kuwapiga risasi za vichwa wote watano na wakafa. “Agrgrrrr” Nilisikia maumivu ya mkuu huyu wa waasi nyumba yangu nia nikageuka kwa haraka na kukuta kiganja chake kikwa kimekatika huku kikiwa kimeshikilia bastola. “Sorry boss, alitaka kukuua” Maulid alizungumza huku akitabasamu. “Safi, eneo lipo salama nina hitaji walinzi wote safari iendelee” “X” Jamaa huyu aliniita kwa sauti ya shida sana kwa maana damu nyinngi zimesha mtoka mwilini mwake. “Naam” “Hujui kwa nini sisi tupo hivi. Akanipa ishara ya kuzima kinasa sauti changu pamoja na simu ninayo mrekodi, nikafanya hivyo kwa maana ukiona adui ana hitaji ufanya hivyo basi ana jambo muhimu ana hitaji kukuambia. Nilicho kifanya ni kuzima kamera ila nikaweka upande wa kurekodia sauti na simu nikaiweka mfukoni mwangu. “Nilizisikia sifa zako, ila hujui ina dili na watu wa aina gani? Nyuma yetu sisi kuna watoa support. Hili tukio la kuvamia wanajeshi wa UN ulikuwa ni mpango wa kusukwa na tulipewa siri zote na kiongozi wenu mkuu wa serikali ya Tanzania”

“Kiongozi gani huyo?” Nilizungumza huku nikichuchumaa chini.

“Huyo muliye ambayana naye leo. Huyo ndio kirusi kikubwa cha utawala kwenye nchi yako. Alihitaji raisi wenu aweze kuuwawa kwa maana alipandikiza marubani walio iteka ndege ya Raisi South Sudan. Alipo ona jaribio la raisi lime shindikana kuuwawa, akahitaji kutengeneza mpango wa sisi kuvamia wanajeshi wa ummoja wa mataifa na makusudio makubwa ilikuwa ni kuwaua wanajeshi wa Tanzania, na ilikuwa leo hii mukija katika eneo hili tuwavamie na kuwau walinzi wake wote na alitusisitiza kusuana na X kwamba ni mtu hatari na wala hakatarajia kama uta kuwepo kwenye msafara huu” Maneno ya mkuu huyu wa jeshi la waasi yakanifanya nianze kuunganisha dote za matukio, kuanzi vile makamu wa raisi alivyo kuwa ana lazimisha tuweze kutumia usafiri magari kutembea katika safari hii iliyo tugarimu siku mbil.

“Makamu wenu wa raisi ana hitaji madaraka ya nguvu na lengo lake ni kuitawala duniani. Hivyo alihitaji wanajeshi wetu watapo vamia msafara wetu basi chini yenu itoa vikosi vije kupambana na serikali ya hapa na wakiishinda basi mimi wanisimamishe kuwa raisi wa nchi hii na kila kitu kiweze kufanyika kwa jinsi anavyo hitaji makamu wako wa raisi” “Haya unayo yazungumza wewe ni kweli?” “Ni kweli, ingiza mkono wako mfuko wa kulia kuna simu ambayo nilikuwa nina wasiliana na makamu wako wa raisin a namba yake ya siri ipo eneo hilo” Nikaingiza kweli na kukuta simu kwa haraka nikiingiza mfukoni mwangu. “Niue wewe kama mwanajeshi mwenzangu. Sinto hitaji niingine kwenye mikono ya wanajeshi wa umamoja wa mataifa kwa maana nita teseka sana. Tafadhali X” Nikamtazama jamaa huyu anaye tokwa na damu kisha nikasimama. Nikatoa simu yangu mfukoni na kuifadhi(save) mazungumzo hayo niliyo yarekodi kisha nikawasha kamera. “Sali salama yako ya mwisho?” Nilizungumza huku nikiwa nina mrekodi. “Sina dini, simuamini Mungu na mimi ndio Mungu, niue kwa maana nina Mbingu yangu hahaaaa” Likacheka kwa sauti iliyo yaa mikwaruzo. Nikamtandika risasi mbili za kichwa mara baada ya kusikia milio ya magari ya msafara wa makamu wa raisi yakisogea eneo la karibu na hapa na ina onyesha wamelitoa lori lililo kuwa lina wazuia wao kupita. Walinzi wakiwa wameongozana na makamu wa raisi pamoja na Maulid wakafika eneo hili. Kila mmoja akashangaa jinsi watu wawili tulivyo fanikiwa kuwaua watu wengi sana. “Hongera sana X” Kila mmoja alinipongeza huku akiwa amejawa na furaha hata, hata makamu wa raisi naye akanipongeza huku akiwa amejawa na tabasamu. Sikuhitaji kumuonyesha utofauti wowote, makamu wa raisi. Nikampigia simu kapteni wa jeshi niliyo kuwa nina wasiliana naye.

“Kapteni tume fanikiwa kuwasambaratisha maadui” “Kweli?” “Ndio” Nikamtajia sehemu tulipo na baada ya dakika kumi magari ya wanajeshi ya umoja wa mataifa yakafika katika eneo hilo. Kila mwanajeshi akashangaa kuona mkuu wa waasi akiwa ameuwawa. “Ni nani ameitekeleza kazi hiyo?” “Mkuu wetu” Walinzi wezangu walijibu. “Hongera sana. Yaani alitupa shida sana huyu” Tukaingia kwenye magari yetu na kuongozana na gari hizi za jeshi huku tukiacha wanajeshi wengine wakiikushanya miili ya waasi hao. Tukafika katika kambi ya jeshi na kupokelewa na mkuu wa kambi hii ambayo ima haribiwa baadhi ya maeneo. “Mkuu” Judy aliniita na nikamuitikia kwa ishara ya macho. Akasimama pembeni yangu huku akitabasamu. “Hongera zako” “Nashukuru” “Aisee wewe kiboko, kama wewe upo hivyo je wezako walikuwa vipi?” “Ahaa, ni akili tu mdogo wangu. Ehee niambie makamu wa raisi kipindi pambano yana endelea ulikuwa katika hali gani?” “Kila mmoja alikuwa kwenye wasiwasi. Tulikuwa tuna sikiliza jinsi ulivyo kuwa una mpa maelekezo Maulid” “Hizi kazi usipo kuwa na akili una kufa” “Ila sijui ni kwa nini makamu wa raisi alikuwa ana lazimisha tupite kwenye eneo hatari kama lile” “Nita muhoji tukirudi nchini Tanzania” “Fanya hivyo kwa maana kidogo wewe una mmudu, ila sisi si una jua” “Usijali” Makamu wa raisi mara baada ya kumaliza kuzungumza na wakuu wa vikosi hivi vya ummoja wa mataifa. Ukaandaliwa mkutano ili azungumze na wanajeshi wa nchi ya Tanzania. Baada ya maandalizi kukamilika makamu wa raisi akanza kuzungumza huku tukiwa tunaimarisha ulinzi kwani ni jukumu letu. “Poleni sana. Ina uma na kusikitisha kuona ndugu zetu wakiwa wameondoka katikati ya mapambano. Sisi kama serikali na pia wananchi kwa kweli tume umia sana kiasi cha kujisikia vibaya sana kwenye mioyo yetu.” Makamu wa raisi akaka kimya huku akionekana ana huzuni usoni mwake.

‘Wewe mzee mbona nina jaribu kujujua alafu nashindwa kukujua?’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikimazama huku akiendelea kuwafariji wana jeshi walio ondokewa na wezao.

“Tukiwa kama nchi ni lazima tulipe na tuna mshukuru Mungu kwamba kiongozi wa waasi hao ame uwawa na vijana wangu ambao nime ambatana nao. Sasa ni wakati wa kusambaratisha vikosi hivyo na visiweze kuonekana kwenye ardhi ya dunia hii” “Jambo jengine nisisite kutoa pongezi zangu kwa vijana wangu Maulid na X ambao kwa kushirikiana kwa pamoja waliweza kumuua mkuu wa vikosi vya waasi. Labda nimpe dakika mbili X azungumze neno kwenu” Makamu wa raisi alizungumza huku akinitazama kwa uso wa furaha. Taratibu nika simama mbele ya wanajeshi hawa.

“Agost 21 miaka minne sasa iliyo pita nchini Pakistani, niliwapoteza wezangu wengu ikiwemo wezangu watatu ambao kwa pamoja sisi wanne tulikuwa tuna unda kundi la X. Nina jua maana ya ambushi, kwani ina waacha mukiwa hamuna jinsi zaidi ya kujikinga na mashambulizi ya adui. Wenu wenu nina imani muta kuwa muna kumbuka shambulizi hilo baya kutoka katika historia ya walinda amani wa umamoja wa Mataifa. Ninacho wasihi musikate tamaa, kwa maana kama ni adui bado yupo msituni, kwani kumuua kiongozi wao, nina imani kuna mwengine ata simama na kuwaongoza hawa. Pale mutakapo nihitaji nita kuwa nanyi na tuta shirikiana bega kwa bega. Asanteni sana” Wanajeshi hawa wakanipigia makofi ya furaha kuliko hata walivyo mpigia makofi makamu wa raisi. Makamu wa raisi akendelea kuzungumza nao na baada ya mazungumzo kuisha, maamu wa raisi akaniita ili tuzungumze sisi wawili tu. “Ndio mkuu” “Kwanza nikupongeze kwa ujasiri wako ulio nionyesha. Ume nifanya nijisikie furaha sana kwenye hii safari japo tupo kwenye kipindi cha kuomboleza” “Usijali, haya ndio matunda uliyo yawekeza kwa kipindi kirefu japo matunda matatu hayakuwepo” “Ni kweli, je ulifanikiwa kumuhisi yule mkuu wa waasi?” Swali la makamu wa waraisi likanifanya nimtazame kwa sekunde kadhaa. “Hapana” “Mmm sawa sawa” Makamu wa raisi akatoa simu yake mfukoni, na kuiminya minya kisha akapiga namba hiyo na nikaanza kusikia mtingisho wa simu(vibration) ya mkuu wa waasi mfukoni mwangu na macho ya makamu wa raisi taratibu akayashusha kwenye mfuko wa suruali yangu eneo linapo ita simu yangu, jambo lililo nifanya nijawe na wasiwasi kidogo kwa maana nina hisi yeye ndio anaye piga.


***


“Ndio muheshimiwa raisi”

Makamu wa raisi alizungumza huku akiiweka simu yake sikioni mwake. Simu ya mfukoni nayo ina endelea kuita, taratibu nika shusha pumzi kwani sio yeye ndio anaye piga.

“Tuna shukuru Mungu, tumefika salama nina imani X aliweza kuwatumia video na picha”

“Huyu hapa una weza kuzungumza naye”

Makamu wa raisi alizungumza huku uso wake ukiwa umejawa na furaha sana. Nikaiweka simu hii sikioni mwangu.

“X tuna shukuru sana kwa huduma yako?”

Niliisikia sauti ya raisi vizuri sana.

“Usijali muheshimiwa ni jukumu langu na pia timu nzima niliyo shirikiana nayo ina paswa kushukuriwa”

“Mukirudi nchini Tanzania wote tuta wafanyia sherehe na wakupandishwa vyeo basi wata pandishwa vyeo”

“Asante sana kwa hilo mkuu”

“Basi tuwatakie safari njema ya kurudi nchini Tanzania”

“Sawa sawa mkuu”

Nikamkabidhi simu makamu wa raisi.

“Muheshimia, tuta ondoka eneo hili majira ya saa kumi usiku”

“Sawa asante”

Makamu wa raisi akakata simu na kuiweka mfukoni mwa kuti lake la suti.

“X”

“Ndio mkuu”

“Ndege tulio jia nayo ita fika hapa kambini majira ya saa saba usiku kisha tuta ondoka usiku huu huu kurudi nchini Tanzania”

“Sawa mkuu”

“Sasa una weza kupata japo usingizi kwa masaa mawili kwani huja lala kabisa Eddy”

“Usijali mkuu nita lala pale nitakapo kamilisha hii kazi”

“Huja choka?”

“Siwezi kuchoka katikati ya uwanja wa mapambano mkuu. Nikichoka adui yangu ata kuja kwa nyuma na kuniua. So ni lazima niwe macho hadi dakika ya mwisho mkuu”

“Safi nina kwenda kwenye hema kupumzika kidogo”

“Sawa muheshimiwa”

Makamu wa raisi akaniacha na kuondoka na walinzi wake wawili ambao aliniambia ana waamini. Nikaitoa simu ya mkuu wa kundi la waasi, nikajikuta nikijawa na mshangao kwa maana simu hii haiwezi kufunguka pasipo kidole(finger print)

“Ohooo”

Nilizungumza huku nikiangaza angaza eneo hili. Nikamuona Maulid akiwa amesimama na baadhi ya wanajeshi akipiga nao stori. Nikamfwata hadi sehemua akipo.

“Dogo njoo mara moja”

Tukasogea pembeni.

“Dogo ile miili ya waasi bado ipo lile eneo au ipo huku?”

“Nina sikia baadhi ya miili imeletwa hapa ukiwemo wa yule mkuu wao”

“Imehifadhiwa wapi?”

“Sijajua kwa maana kambi hii ni kubwa sana, ila ngoja niwaulize hawa wanajeshi”

Maulid akawauliza wanajeshi hawa kisha akarudi nilipo. Tukaondoka eneo hili na kuelekea kwenye hema moja kubwa ambapo ndipo ilipo miili ya waasi hao baadhi.

“Kwani mkuu uta tafuta nini?”

“Kuna kitu nina kihitaji”

Tukaingia ndani ya hema hili, kutokana na mwanga hafifu wa taa iliyopo hapa, nikatoa simu yangu mfukoni na kuanza kumulika mulika maiti za wanajeshi hawa waasi.

“Nisaidie kumtafuta yule mkuu wao”

“Sawa”

Mimi nikaelekea kulia na Maulid akaelekea kushoto huku tukitafuta maiti ya mkuu wao.

“Hii huku boss”

Maulida alizungumza na kunifanya nimfwate sehemu alipo.

“Fuc**”

“Kuna nini mkuu?”

“Mbona amekatwa viganja vyake?”

Maulid naye akashangaa kwa maana alikuwa hajalistukia jambo hilo.

“Labda walikuwa na hasira naye”

Nikashika mikono yake iliyo katwa na nika gundua kwamba ame katwa muda si mrefu.

“Maulid huyu amekatwa muda si mrefu”

“Kweli mkuu?”

“Ndio”

“Kwani mkuu una tafuta nini?”

“Nita kuambia nikikamilisha uchunguzi wangu”

Tukatoka katika heme hili.

“Yupo wapi Judy?”

“Niliachana naye muda fulani, nina hisi yupo na wanajeshi wa kike ana zungumza nao.

“Tumtafute kuna kazi nina hitaji niwapatie”

“Sawa”

Tukazunguka kwenye mahema kadhaa na tukafanikiwa kumpata Judy.

“Sikilizeni madogo kuna mambo ambayo yana endelea na muna paswa kuyafahamu. Jambo lenyewe ni jambo hatari sana na ambalo lina weza kutupelekea kuingia kwenye matatizo.”

Maulid na Judy wakanitazama usoni mwangu kwa mshangao.

“Una maanisha nini mkuu”

Judy aliuliza huku macho yakimtoka.

“Kabla ya mkuu wa waasi kufariki kuna siri moja aliweza kunipatia siri ambayo hata mimi mwenyewe niliduwaa ili kuupata ushahidi dhaidi niliweza kurekodi mazungumzo yake”

Tukasimama eneo ambalo wanajeshi hawapitipiti. Nikatoa simu yangu mfukoni na kuwasikilizisha mazungumzo niliyo yarekodi dakika ya mwisho kabla mkuu wa waasi hajafariki duniani. Maulid na Judy wakastuka sana huku macho yakiwatoka.

“Ina maana makamu wa raisi ndio yupo nyuma ya hili jambo?”

Maulid alizuliza huku akiwa amejawa na mshangao mkubwa sana.

“Ndio”

“Mungu wangu, sasa mkuu tuna fanyaje?”

“Kila mtu nina muingizia hii sauti kwenye simu yake. Endpo kuta kuwa na jambo lolote lita nipata basi hakikisheni kwamba hii rekodi ana ipata muheshimiwa raisi pale tu mutakapo ona nime pata shida yoyote kwa maana nimesha anza kuona mwisho mbaya kati yangu na huyu mzee”

Nikawaingizia Maulid na Judy audio hiyo ya sauti.

“Nina simu ya mkuu yule, simu hii ndio ita tupatia ushahidi wa kila jambo la makamu wa raisi, kuanzia mazungumzo yake, meseji na kila kitu. Tatizo ni kwamba ina funguliwa kwa finger print.”

“Okay sasa mkuu ndio nina kuelewa. Ndio maana wamekata vinganja vyake?”

“Ndio”

“Nani amekatwa viganja vyake?”

Judy aliuliza huku akitutazamakwenye nyuso zetu.

“Tulikuwa tuna itafuta maiti ya mkuu wa kundi la waasi. Nilikuwa nina hitaji kuifungua simu yake kwa kidole chake kimoja wapo, ila kwa bahati mbaya tumeweza kukuta viganja vyake vime katwa muda si mrefu”

“Mmmm ukiona hivyo mkuu basi tambua kuna watu katikati yetu wana fahamu mchezo mzima?”

Judy alishauri.

“Yaa, ndio maana nime watumia hizo audio kwa maana sasa hivi hatufahamu adui halisi ni nani kwani tuna sakana humu kwa humu”

“Mkuu hapa cha kushauri ina bidi tukulinde wewe”

Maulid alizungumza.

“Ni wazo zuri, ila musijali, hakuna ambaye ana weza kunidhuru. Kikubwa tujifanye kama hatujui kilicho tokea”

“Sawa mkuu”

“Si muna ripoti ya muda gani tuna ondoka?”

“So kuweni makini”

Nikaachana na Judy pamoja na Maulid. Nikaelekea katika hema alipo makamu wa raisi. Nikamkuta na baadhi ya wakuu wa jeshi la Tanzania na umoja wa mataifa wakipata mvinyo.

“Karibu X”

Makamu wa raisi alizungumza, nikavuta moja ya kiti cha chuma na nikaketi.

“Kijana kwa nini usijaribu kurudisha kikosi chako cha X ukawa na timu mpya?”

Mkuu mmoja alizungumza.

“Sio rahisi kama unavyo dhani kwa maana wale nilikuwa ni ndugu zangu kabisa na tulifundishwa mambo mengi kwa wakati mmoja na kwa muda mfupi. Hawa wengine wana jaribu kupita pita huku na kule bado sijaipata ile ladha ninayo ihitaji na isitoshe hii ndio kazi yangu ya mwisho hivyo sinto rudi tena kazini”

“Ila X umri bado una ruhusu kwa nini usiendelee kulitumikia taifa lako badi una hitajika?”

“Muda wangu umesha kwisha sasa ni muda wa kuanzisha familia, naamini mkuu hapa ana fahamu kwamba nime oa wiki iliyo pita”

“Hongera sana kwa kufunga ndoa”

“Nina shukuru”

Tukazungumza mambo mengi na wakuu hawa wa majeshi. Muda wa sisi kuondoka ukafika, tukaagana na wanajeshi wote huku makamu wa raisi akiwapa neno la kuwafariji wanajeshi wote. Tukaingia kwenye ndege tuliyo jia nayo nchini hapa DRC na safari ya kurudi nchini Tanzania ikaanza.

“Ohoo asante Mungu tume rudi salama”

Nilizungumza huku nikimtazama makamu wa raisi.

“Ni kweli, huwa nikiwa na wewe huwa siogopi kabisa. Ila Eddy huwa kila ninapo isikia kauli yako ya kwamba una acha kazi basi moyo wangu huwa una poteza amani kabisa”

“Usijali mkuu, ndio maisha. Kila jambo lina mwanzo na mwisho wake”

“Ni kweli”

“Mkuu ule mpango upo?”

“Mpango gani?”

“Tulio zungumza kwenye gari, juu ya DRC?”

“Tuna kosa nguvu ya kupiga hatua mbele kwani tume weza kuwawahi waasi na kumuua kiongozi wao. Hivyo nchi kama hichi tume pewa pongezi na vyombo vya habari duniani vimesha anza kutangaza juu ya kifo cha mkuu wa waasi wa nchini DRC”

“Wana jeshi wetu nao vipi?”

“Milii yao tuta ipokea kesho kutwa nchini Tanzania”

“Familia zao nazo zime achanjwe?”

“Ummoja wa mataifa wame toa kwa kila familia dola laki moja na nusu huku nchi kama nchi tuta toa milioni mia moja kwa kila familia”

“Ahaa sawa sawa hapo kidogo familia zita weza kujikimu kwenye kipindi hichi”

“Ni kweli”

Safari ikatuchukua masaa kadhaa. Majira ya saa nne asubuhi, tukatua katika uwanja wa jeshi la anga jijini Dar es Salaam. Tukaingia kwenye gari za makamu wa raisi zilizo kuja kutuchukua na moja kwa moja tukaelekea ikulu. Tukapokeleza ikulu vizuri sana na raisi pamoja na viongozi wengine wa jeshi.

“Hongera sana X”

Raisi alizungumza huku akinikabidhi mkono wake.

“Nashukuru sana mkuu”

“Kwa kweli, nchi ime pata sifa kwa ajili yako na habari zako zime samba kote kwenye vyombo vya habari na matumaini mapya ya wananchi juu ya kundi la X sasa yame pamba moto kwenye mitandao ya kijamii.

“Ila nina imani sura yangu haijawe kwenye mitandao?”

“Ndio na kila mmoja ana uliza nani ni X?”

“Ni jambo zuri mkuu. Samahani nina weza kwenda nyumbani sasa kwa maana nina imani mke wnagu ana nisubiria sana”

“Ndio una weza kwenda, ila kumbuka kwamba kesho usiku kuta kuwa na sherehe ya kuapandisha vyeo na kesh kutu tuta ipokea miili ya wapiganaji wetu”

“Nime kuelewa mkuu”

Nikaachana na raisi, nikawatafuta Maulid na Judy.

“Oya madogo tuondokeni, kuna sehemu nahitaji niwapitishe”

“Sawa boss”

“Eddy Eddy”

Maria aliniita huku akinikimbilia. Ikanibidi nisimame na kwa haraka akanikumbatia huku akihema kifuani mwangu.

“Hei kuna watu”

“Sijali, siwezi kuendelea kuficha hisia zangu ikiwa nilisha kueleza”

Maulid na Judy wakakonyezana kisha wakasogea pembeni na kuniacha mimi na Maria.

“Eddy nina kuomba please unipatie hata siku moja tu ya kuupata utamu wako”

“No no no no, nikikupa utamu wangu uta kolea na mwenzako nimesha oa”

“Najua ila nita muheshimu mke wako na ndoa yako”

“Maria hapa kichwa changu hakipo okay. Naomba nielekee home kisha baada ya hapo tuta wasiliana, nina namba yako na una namba yangu ila usipige hadi mimi nikupigie”

“Sawa bwana Eddy”

“Ila una kajoto katamu”

Nilimnong’oneza Maria kisha tukaachiana huku akitabasamu. Tukaingia kwenye gari na wadogo zangu hawa wawili na safari ikaanza. Nikampigia simu Willy.

“Kaka”

“Upo wapi?”

“Nipo home”

“Usitoke nina kuja na wageni?”

“Umesha rudi nchini Tanzania?”

“Ume juaje kwamba ume ondoka?”

“Kaka umesahau mimi ni nani, nina jua na video uliyo ituma ikulu ninayo”

“Dogo boya kweli wewe una taka kuniambia kwamba ume hack security stsyem ya ikulu”

“Yaa siwezi kukuficha”

“Sawa tuna kuja”

Tukafika Mburahati, nikaliacha gari mbele ya duka la Mangi na akashangaa kutuona tume valia suti nyeusi na mashati meusi. Kitu kingine kilicho mshangaza ni jinsi earphone tulizo zivaa masikoni mwetu. Sikutaka kumsalimia kama ninavyo msalimiaga siku nyingine, nikampa ishara ya salamu kisha tukaendelea kukatiza kwenye vichochoro vya nyuma hizi zilizo kaa bila mpangilio maalumu.

“Huku mkuu umepajuaje?”

Judy alizungumza huku tukiruka madimbwi ya maji machafu.

“Mdogo wangu Dar es Salaama nzima hakuna sehemu nisiyo ijua, kabla ya kuwa X nilikuwa kibaka, mdokozi hivyo sehemu zote hizi nina zijua. Tukafika nyumbani kwa Willy na kuingia nyumbani kwake. Nikawatambulisha Judy na Maulid kwa Williy.

“Huyu ndio yule aliye kuwa ana nitumia location ya shemeji yangu. Yupo very smart kwenye maswala ya I.T”

“Ohoo hongera sana dogo”

“Nina shukuru”

Nikamkabidhi Willy simu ya mkuu wa kundi la waasi wa DRC na nikampa maelezo.

“Nina imani kwamba ita funguka hii simu?”

“Hiyo ni kazi ndogo kwangu”

Willy akaanza kuifanyia kazi hii iphone 7+. Haikuchukua muda mrefu simu akafanikiwa kuifungua. Tukaanza kutazama meseji zilizo tumwa, ramani za kambi ya wanajeshi wa umoja wa mataifa.

“Ohooo Mungu wangu?”

Willy alizungumza huku akitingisha kichwa.

“Nini?”

“Kaka hawa jamaa wana contection kubwa a wana kundi kubwa sana, ukiachana na wao tu wa DRC hii ndio listi ya group zima na lina tawaliwa na mkuu”

Willy akahamisha listi ya majina ya kundi zima liitwalo Scorpion, kwenye tv kubwa iliyopo eneo zima. Kundi hili lina ongozwa na makamu wa raisi huku likiwa lina dhamini vikosi vya kigaidi na waasi ulimwenguni mwote, ikiwemo na waasi walio teka ndege ya raisi. Jambo hili likaningyong’onyeza na kujikuta nikikaa kwenye sofa huku nikiatazama Maulid na Judy ambao nao wana onekana kushangazwa na jambo hilo.



“Makamu wa raisi!?”

Judy aliuliza huku akiwa amejawa na mshangao mkubwa sana.

“Ndio kinacho onekana hapa sister”

Willy alijibu huku akimtazama Judy usoni mwake.

“Nashindwa kuelewa”

Nilizungumza huku nikiwa nime inamisha kichwa changu chini

“Kwa nini mkuu?”

Maulid aliniuliza.

“Kama makamu wa raisi ndio anaye miliki huo mtandao wa Scorpion sijui nini. Kwa nini alihitaji niweze kurudi kazini na tena kwenda kumuokoa raisi?”

“Hapo napo kuna mtihadi mkuu. Kama yeye ndio aliye mteka kwa nini atutume tuka muokoe”

Judy naye alihoji.

“Nina hisi kwamba kuta kuwa na kitu ndani ya hili jambo na isitoshe kama raisi ana tekwa tutambue ni kwamba viongozi wote wa ngazi za juu wata fahamu hususani wa usalama. Hivyo nahisi ilikuwa ni ngumu kwa yeye kuto ikamilisha kazi yake hivyo akaamua kutuagiza sisi”

Maulid alitengeneza pointi ambayo kidogo ikaanza kunipa majibu ambayo japo ni magumu.

“Ina bidi tufahamu magaidi walikuwa wana hitaji nini nje ya kutaka pesa na kumshinikiza raisi wa Tanzania kujitoa kwenye uwenyekiti wa kamati ya upatanishi wa Sudan ya kusini”

Nilizungumza huku nikiwatazama wezangu kwenye nyuso zao.

“Ni kweli kaka”

“Na pia lazima tujue ni nani aliweza kuhack system nzima ya ndege ya raisi hadi ika potea angani na mwisho wa siku ipatikane kule kule Sudan Kusini ikiwa ilisha onekana imepaa kwa ajili ya kuja Tanzania. Mbili katika idadi ya walinzi wa raisi walio kufa, ni mmoja tu na rubani mmoja ndio wali miss kwenye ile orodha. Inavyo onyesha hao ndio wasaliti na ile siku tuna kwenda kuokoa kambini hawakuwepo”

Niliendelea kulichambua taratibu tukio zima.

“Inavyo onesha jukumu lao lilikuwa ni kuifikisha ndege hiyo kwa magaidi kisha wao wakajiweka pembeni”

Maulid naye alichangia mada hii.

“Ila mlinzi mmoja ana wezaje kuwaua walinzi zaidi ya arobaini ambao wana mlinda raisi?”

Judy alihoji.

“Dogo una weza kutupatia rekodi za kamera zilizo rekodi tukio zima ndani ya ndege ya raisi”

“Broo hiyo ni hatari sana”

“Kwa nini?”

“Baada ya tukio lile kila kitu kiliweza kuboreshwa kwenye ndege ya raisi hivyo now mtu akijaribu ku hack chochote ndani ya ndege in akula kwake ni lazima wafahamu ni sehemu gani alipo”

“Willy acha masihara mdogo wangu, ina maana una weza kuhack ikulu ushindwe ku hack ndege ya raisi”

“Je muna code za ndege hiyo kwa maana code zake ana zijua raisi tu”

“Code hizo kazi yake ni nini?”

Maulid aliuliza.

“Ndege ya raisi, mfumo wa kiteknolojia wa ikulu pamoja na mfumo mzima wa kulipulia mabomu ya nyuklia ambayo nchi yetu ina vimiliki, kuna code ambazo ni raisi pekee yake ndio anazijua. Hii ya ikulu ni rahisi sana kuifahamu kwa maana kuna wafanyakazi wengi sana, niliweza kuhack computer ya chief secretary na nika fahamu kila jambo la ikulu na ikwa ni rahisi kujua kinacho ingia na kutoka katika ikulu. Ila hizi mbili ni ishi ndugu zangu”

“Williy nime pata wazo”

Nilizungumza.

“Nakusikiliza kaka”

“Kuna video ambazo makamu wa raisi alinionyesha kwenye tablate je una weza kuingia system ya ikulu uka pata video hizo”

“Ninazo”

Willy akatuwekea video fupi ambayo ilitumwa na magaidi wakitoa maagizo hayo kwa serikali ya Tanzania na walihitaji wayatekeleze na yasipo tekelezwa wata muua raisin a mateka walio salia ambao ni wafanyakazi wanao ambanata na raisi kila anapo kwenda. Tukaitazama video hiyo kwa mara nne mfululizo ila hatukuweza kupata kitu cha kutufanya tujue nyuma ya pazia iliwezekana vipi hadi mlinzi mmoja wa raisi akawaua walinzi wote.

“Hembu rudisha nyumba kidogo Williy”

Judy alizungumza na Willy akairudisha video hiyo nyuma kidogo.

“Isimamishe”

Judy alizungumza huku sote tukitazama.

“Mume ona huyu mtu aliye simama nyuma ya kamera”

Judy alitoonyesha mtu huyo kwa kupitia kioo cheusi kilicho mnasa akiwa amesimama huku mbele yake akiwepo raisi pamoja na gaidi amzungumzaji.

“Mumeona ame vaa kizuia gesi?”

Judy alituonyesha na kumfanya Willy kuikuza picha hiyo na sisi sote tukaweza kuona anacho tuonyesha.

“Okay ina maana walivaa vizui gesi, wakafungulia gesi ya usingizi na watu wote wakalala na ikawa njia raisi kwa wao kuwaua walinzi wote?”

Nilizungumza huku sote tukiwa tumepata jibu kamili la kipi kilitokea siku hiyo

“Yaa”

“Willy una weza kuufwatilia mtandao huo wa Scorpion ukajua unaendeshwa endeshwa vipi?”

Nilimuuliza Willy na akaanza kuifanya kazi hiyo ambayo haikumaliza hata dakika tano, tuka pata maelezo mengine ya siri.

“Hawa Scorpion kazi yao ya kwanza ni kutengeneza ma Expendable people, katika list ya watu hao X mupo”

Nikastuka sana mara baada ya Willy kusoma maandishi hayo.

“Usishangaee kaka hii hapa, nyinyi ndio kikundi cha tatu na cha mwisho kutengenezwa na hao Scorpion. Kikundi cha kwanza kilikuwa kina itwa SIX. Kilikuwa na wanajeshi wenye asili ya Rusia na wanajeshi hawa walifanya oparesheni ishirini na mbili na oparesheni ya ishirini na mbili wakauwawa kwa shamulizi la gafla”

Mapigo yangu ya moyo yakaanza kunienda mbio mara baada ya kumsikia Willy akisoma maandishi hayo. Jashi likaanza kunichuruzika usoni mwanangu, na kujikuta nikivua koti japo ndani hapa A/C(Air condition) ni kali sana.

“Hicho kikisi kiliweza kuwaingizia kiasi cha dola za kimarekania bilioni mbili na itendaji wao wa kazi ilikuwa kushirikiana na vikosi vya umoja wa mataifa katika kuwasaka magaidi.”

Willy akanifana tumbo langu kuni nguruma kwa njaa huku nikihisi kichwa kama kikianza kupandwa na maruhani yangu ya ukatili ambayo ni kwa miaka mingi sana yalisha potea kichwani mwanangu pale nilipo amua kuwa mtu mzuri na hata siku mbili hizi nilizo waua magaidi ilikuwa ni katika moja ya njia ya kujilinda na kutimiza majukumu yangu.

“Japa mchezo wanao ufanya, wana unda kikosi cha watu hatari, kina fanya kazi kwenye mashirika makubwa kama CIA, FBI na umoja wa mataifa na vikosi hivyo huwa vina fanya kazi ambazo ni ngumu kwa vikosi vingine kuweza kuzifanya na pesa wanayo lipwa kutoka hayo mashirika wana tenga kiasi kidogo na kuwalipa wanajeshi hao ambao huamini wana fanya kazi chini ya serikali za nchi zao”

“Willy endelea mbele acha maelezo mengi”

Nilizungumza huku nikikunja kumi mikono yangu yote mwili huku kila moja akinitazama kwa macho ya wasiwasi kwani tayari nimesha anza kupandwa na hasira.

“Kikosi cha pili ni PIG kilianzishwa nchini Africa kusini, ila hakikufanya vizuri, kilikuwa na wanajeshi wanane na waliuwawa mara tu ya kufanya oparesheni ya kumuua raisi wa Msumbiji na wao waliuwawa kwa shambulizi. Waliingiza kiasi cha dola milioni mia”

“Kikosi cha tatu ni X ambacho ndio cha mwisho katika mpango wao. Kikosi hicho ni kutoka nchini Tanzania na kilikuwa na wanajeshi wa nne na picha zenu hizi hapa kaka”

Hata sikuwa na haja ya kutazama picha hizo na nilicho kifanya ni kumpa ishara Willy kuendelea kusoma malekezo hayo.

“Ahaa kikosi cha X kiliweza kuwaingizia dola za kimarekani bilioni kumi kwa oparesheni zote zilizo fanywa na kikosi hicho. Pia baada ya kazi yao kuisha, ukafanywa mpango wa wao kuuwawa nchini Pakistani na kiliuwawa kwa shambulizi la gafla lililo fanywa na magaidi hivyo hapa rekodi zao zina onyesha walikufa wanajeshi wote wa kundi la X na walio ambata nao”

Nikanyanyuka kama mzimu utokao kaburini. Nikachomoa bastola yangu kila mtu akastuka, uso wangu umesha chafukwa kwa hasira. Moyo wangu umeshatawaliwa na jini la mauaji, huku namfsini mwangu nikiichora picha ya makamu wa raisi jinsi alivyo tuchukulia sisi kama watoto wake wa kuwazaa na kutupeleka kwenye mafunzo magumu ila kwa umoja wa marafiki zangu tuliweza kuyamudu na mwisho wa siku ana kuja kutua yeye mwenyewe.

“Mkuu una taka kwanda wapi?”

Judy aliwahi kunizuia njia kwa kusimama mbele yangu.

“Nina kuomba upite”

“No siwezi kama una take kwenda kufanya kitu chochote cha kijinga niue kwanza mimi”

“Na mimi pia niuae”

Maulid naye alisimama mbele yangu huku wote wakinikazia macho. Nikaikoki bastola yangu na kuwanyooshea kwenye nyuso zao huku mikono ikinitetemeka kiasi cha kuhisi uchungu mithili ya mwana mama anaye jifungua leba. Macho ya Willy yakabaki kututazama tu.

“Mkuu tuna tatambu kwamba una pitia kipindi kigumu. Ila fikiria familia yako, fikiria mke wako fikiria maisha yako ya ndoa. Yana thamani kubwa sana zaidi ya hicho unacho taka kwenda kukifanya”

Maulid alizungumza huku akinitazama machoni mwangu.

“Una mke mzuri mkuu, ana hitaji kupata mtoto mzuri kutoka kwako. Hembu fikiria hilo’

Judy alizungumza huku akwia amenishika kufuani mwangu.

“Mkuu haya mambo tusikurupuke tutulie na tuta pata njia ya kulipa kisasi taratibu.”

Maulid alizungumza huku akinitazama usoni mwangu. Nikavta pumzi nyingi kisha nikaishusha pumzi hiyo taratibu huku nikiwa nina tafakari nini cha kufanya.

“Naomba maji ya baridi”

Nilimuambia Willy na kwa haraka akananyuka na kufungua friji yake ya hapa sebleni, akatoa chupa ya maji ndogo na akanirushia. Nikaidaka na kuifungua, nikaanza kunya maji haya mfululizo hadi yakaisha. Siku zote hasira yangu huwa ina tulizwa na maji ya baridi na Willy hilo huwa ana lijua kwani sio mra yake ya kwanza kuweza kuniona nikiwa nime kasirika. Nikakaa tena kwenye sofa huku nikiichomeka bastola yangu sehemu nilipo itoa na kuwafanya Judy na Maulid nao kukaa kwenye sehemu zao walipo kuwa wamekaa.

Ukimya ukatawala ndani hapa huku kila mtu akisibiri kusikilizia ni kitu gani nita kizungumza kwao.

“Willy”

“Ndio kaka”

“Niandalie listi nzima ya hao Scorpion, nitumie kwenye akaunti yangu. Sasa hivi nina hitaji kwenda kuonana na mke wangu”

“Sawa”

“Vipi nyingi wengine muna baki hapa au tuna ondoka wote”

“Ngoja tuka jipumzishe na sisi”

Tukaagana na Willy na kuondoka hapa nyumbani kwake. Tukarudi tulipo liacha gari, tukaingia na kuondoka eneo hilo, nikampitisha Judy na Maulid kila mtu nyumbani kwake, kisha moja kwa moja nika elekea nyumbani kwangu. Nikafunguliwa geti na walinzi nilio waacha siku nina ondoka. Mke wangu akatoka kwa kasi ndani na kunirukia kwa furaha mara baada ya kushuka kwenye gari.

“Karinbu sana nyumbani mume wangu”

Cauther alizungumza kwa furaha iliyo pita maelezo.

“Nashukuru mke wangu”

“Mbona hujaniambia kwamba una rudi mume wangu, nikaandaa madikodiko unayo yapenda?”

“Najua wewe fundi mke wangu, muda wowote ule una niandalia mambo matatamu”

“Sawa mume wangu, kama una njaa ngoja fasta nikuandalie msosi”

“Noo nahitaji kwanza msosi wa mwili”

Mke wangu akatabasamu kwa maana anatambua kitu ninacho kipenda kuliko vitu vyote ni Sex. Nikaingia naye chumbani huku tukivuana nguo. Hadi tunafika kitandani kila mmoja hana nguo, nikaanza kumshuhulikia mke wangu huku mawazo ya makamu wa raisi yakinitawala sana kichwani mwangu. Matukio ya kuuwawa kwa rafiki yangu yakanitoa nje kabisa ya mfumo mzima wa kufanya tendo la ndoa hadi nikajikuta jogoo wangu akilala kabla ya hata mechi kumalizika.

“Honey vipi?”

Mke wangu aliniuliza huku akinitazama jinsi ninavyo mwagikwa na jasho usoni mwangu huku mikono ikinitetemka. Taratibu nikajito mwilini mwake kwa maana tulikuwa kwenye mkao wa kifo cha mende. Nikakaa kitako kitandani na kumfanya mke wangu naye kukaa hivyo.

“Mume wangu una tatizo gani?”

“Nina mawazo sana”

“Pole mume wangu. Twende tukaoge nikupigie, ule kisha ulale”

Nikamtazama kwa sekunde kadhaa Cauther.

“But am sorry baby”

“Usijali mume wangu. Najua lazima uta kuwa una mawazo na kazi unayo ifanya ni ngumu sana. Hivyo usiwe na wasiwasi katika hilo”

“Ila umekojoa?”

“Mara ya kwanza ila hii ya pili bado”

Cauther alizungumza kwa sauti laini ya kudeka kwa maana amesha zoea huwa nikimpa show zina kuwa ni za kibabe, goli langu moja kwake ni magoli kuanzia mawili na kuendelea. Tukanyanyuka na kuingia bafuni, tukaoga kisha akelekea jikoni kuandaa chakula. Nikajilaza kitandani na usingizi ukaanza kuninyemelea nyemelea. Simu yangu ikaanza kuita, nikanyanyuka na kuichukua juu ya meza ilipo wekwa na mke wangu. Nikaitoa mfukoni na kukuta ni namba ngeni.

“Haloo”

Nizungumza huku nikiiweka simu yangu sikioni. Mtu aliye nipigia simu hakuzungumza chochote zaidi ya kukata simu, nikaitazama namba hii kisha nikaendelea kuutafuna usingizi kwani ni kwa siku karibia tatu sijalala.

“Ume lala mume wangu, twende ukale au uta kula ukiamka”

Niliisikia sauti ya Cauther kwa mbali.

“Mmm”

“Twende tukale”

Nikashusha pumzi huku taratibu nikijeuza. Nikanyanyuka na tukaelekea sebleni, tukapata chakula hichi cha mchana kisha nikarudi chumbani na kuendelea na usingizi wangu ambao ume nikamata kisawa sawa.

Nikakurupuka usingizini huku nikihema sana, ndoto za wezangu, nikiwashuhudia wakiwa wamevalia mavazi yao ya kijeshi huku wakimwagikwa na damu katika vichwa vyao huku wakinikimbiza imenistua sana. Nikatazama chumbani na sikumuona Cauther. Nikafungua dirisha na kuchungulia nje na nikaona giza likiwa lime tawala anga tayari. Nikashuka kitandani, nikachukua moja ya pensi ambayo mke wangu ameniwekea kwenye sofa, nikaivaa na nikatazama saa iliyopo katika simu yangu na kugundua ni saa tatu usiku.

“Baby”

Niliita huku nikitoka chumbani hapa. Sebleni sikuweza kumkuta Cauther, nikaelekea jikoni napo sikuweza kumkuta, ila mazingira ya nyumba yame pangwa vizuri sana. Nikatoka nje na kuwakuta walinzi huku gari langu likiwa halipo.

“Mkuu habari”

“Salama, amekwenda wapi huyu bibie”

“Alitoka majira ya jioni alidai kwamba baba yake amempigia simu”

“Baba yake?”

“Ndio, ila aliseme ukiamka tukujulishe umpigie simu”

Nikampigia Cauther, simu yake ikaanza kuita baada ya muda ikapokelewa.

“Mume wangu samahani kwa kuondoka nyumbani pasipo kukuambia kitu chochote”

“Usijali, upo wapi?”

“Nipo nyumbani kwa wazazi. Baba ameitisha kikao cha galfa, nikaona nikikuamsha ita kuwa sio vizuri ikiwa ume choka, ila samahani sana mume wangu”

“Sawa, kikao kime kwisha au bado?”

“Bado hapa nimeingia chumbani ili kuzungumza nawe”

“Kikao ni cha wema au?”

“Ana gawa mirathi yake kwa wanawe wote. Tutazungumza baadae mume wangu”

“Kwani afya yake sio nzuri?”

“Ime tengemaa ila sijajua ni kwa nini ana gawa”

“Okay nina toka mara moja. Utakapo kuwa una toka nyumbani nipigie simu nikuambie nipo wapi kisha nikupitie”

“Sawa mume wangu”

“Nikakata simu, nikarudi ndani, nikavaa tisheti pamoja na raba, nikachukua kiasi cha pesa kidogo na kutoka ndani kwangu. Nikawaba walinzi, nikatoka nje, nikasalimiana na majirani kadhaa kisha nikakodisha pikipiki kisha nikampigia simu Maria.

“Upo wapi?”

“Nipo kwangu”

“Nina kuja”

Nikaelekea hadi Kimara mwisho ambapo ndipo anapo ishia Maria. Akanikaribisha nyumbani kwake kwa furaha.

“Una ishi na nani kwa sasa?”

“Na mdogo wangu na muda huu ndio nime rudi kutoka kazini”

“Sawa, nime kuja kwa jambo moja”

Maria akakunja nne kwenye sofa lake na kukifanya kisketi chake kupanda juu kiasi na kuyaacha mapaja yake wazi ikiwa ni mtego tosha wa kunitamanisha.

“Nina hitaji kufahamu mulivamiwa vamiwa vipi ndani ya ndege hadi ikatekwa”

Maria akakaa kimya huku akinitazama machoni mwanangu kisha akaka kaswa.

“Eddy hilo swali, nimesha lijibu kwa vyombo vya upelezi wa jambo hili nawe una lirudia”

“Nina maana yangu”

“Okay mara baada ya kupaa kutoka katika nchi ya South Sudan. Kama baada ya dakika kumi hivi ndege ikiwa hewani, tulianza kuhisi usingizi na tulilala fofofo. Sijui nini kilitokea, ila tulivyo kuja kuzinduka, tukajikuta tukiwa tume fungwa kamba huku tukiwa chini ya wale watekaji huku walinzi wengi wa raisi wakiwa wame uwawa”

Maeleo ya Maria yakaanza kunipa picha halisi ya kile tulicho kuwa tuna kihisi, taratibu nika jiapiza moyoni mwangu kwamba nita ifatwilia kesi hii na kundi zima la Scoripion na nita wasambaratisha mmoja baada ya mwengine kimya kimya hadi wakija kustuka basi wata jikuta wakiwa wamesha kwisha.



“Nashukuru Maria nina ondoka sasa”

“Khaaa Eddy!! Yaani kutoka umbali wote huo umekuja kuuliza swali hili na hata maji ya kunywa hujanywa hembu acha hizo”

“No kuna sehemu nilikuwa nina toka, nikaona nipitie hapa kwako, ipo siku nita kuja kula na kunywa na kukaa siku nzima”

“No Eddy. Hii nafasi niliisubiria kwa kipindi kirefu sana. Nilimuheshimu rafiki yangu ndio maana sikutaka kufunguka kwako, ila leo Eddy nina kuomba unipatie hata kidogo”

Maria alizungumza kwa sauti iliyo jaa mahaba mengi sana huku akikimbilia mlangoni, akafunga mlango wa kutokea nje na kunza kufungua vifungo vya shati lake na akabakiwa na siridia. Akavua suruali yake ya kitambaa na akaitupia pembeni na akabakiwa na skintaite na sidiria.

“Ila Maria kumbuka kwamba nina ndoa na haijamaliza hata mwezi”

“Ukinitomb** sasa hivi uta kwenda kumuadithia yule muarabu koko wako kwamba ume nitomb**”

Maria alizungumza kwa kukasirika kidogo na kunifanya nitabasamu.

“Sikia, muheshimu mke wangu, sinto hitaji hisia zako za mapenzi ziweze kumshusha thamani mke wangu au kumdharau kwa hali iliyo yoyote tumeelewana?”

“Nisamehe Eddy”

Maria alizungumza kwa sauti ya upole na iliyo jaa unyonge mwingi sana. Taratibu akanikalia mapajani mwanagu huku akiifungua sidiria yake na akaanza kunigusa gusa na maziwa yake makubwa kiasi usoni mwangu.

“Ngoja kwanza”

Nilizungumza kisha nikaivua pete yangu ya ndoa na kuiingiza kwenye mfuko wangu wa pensi hiliyo ivaa kwa maana siwezi kufanya usaliti huku pete yangu ya ndoa ikiwa kidoleni mwangu. Tukaanza kunyonyana denda huku kila mmoja akisikilizia fukoto la mahaba lilinalo tawala katikati yetu. Simu yangu ikaanza kuita.

“Ngoja kwanza”

“No usipokee bwana”

Maria alizungumza huku akinishika mkono wanguwa kushoto ambao una hitaji kutoa simu yangu mfukoni.

“No inaweza kuwa ni simu muhimu”

“Eddy”

“Ngoja”

Ikabidi nitumie ukali kidogo na nikaitoa simu yangu mfukoni.

“Shiiiiii”

Nilimuambia Maria kwani ni simu ya mke wangu Cauther.

“Honey”

Nilianza kuzungumza mara baada ya kuipokea simu hiyo.

“Baby una weza kuja nyumbani kwetu?”

“Sasa hivi?”

“Ndio mume wangu”

“Kuna nini?”

“Kuna jambo moja baba ana omba msaada. Nilisha mueleza kila kitu kuhusiana na wewe samahani sana mume wangu, ila ameamini kwamba wewe una weza kumsaidia”

Nikashusha pumzi kidogo.

“Ndugu zako wote wapo?”

“Wote wapo”

“Sawa nina kuja, ngoja nikodi bodaboda”

“Sawa”

Nikakata simu na kuirudisha mfukoni mwanangu.

“Nahitaji kwenda”

“Nilijua tu Eddy, ona sasa umeniacha nina nyeg** zangu una hisi unacho nifanyia ni jambo zuri ehee?”

Maria alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake.

”Ila Maria, kwani nime kufa, ipo siku tuta kutana na tuta maliza hapa tulipo ishia. So wewe vumilia hadi siku hiyo nitakapo kuwa vizuri”

“Haki ya Mungu Eddy, umenikera”

“Usijali”

Nikanyanyuka na kuivaa pete yangu kidoleni.

“Aisee huja niachia marangi ya midomo huku nisije kwenda kuumbuka”

“Sijui mimi”

Maria alizungumza kwa chuki. Nikatabasamu tu kwa maana nina waelewa wanawake hususani wakiwa kwenye hali ya muhemko wa kimapenzi tena wakiwa wameachwa na nyeg** zao. Nikatoa simu yangu na kuweka upande wa kamera. Nikajitazama eneo zima la usoni mwangu na shingoni na kujiona nipo salana na sina alama yoyote ya lipstick au love bite.

“Hei nifungulie basi”

Maria akanipandisha na kunishusha kisha akasimama na kuanza kutembea kwa hasira hadi mlangoni akafungua na kuufungua mlango.

“Toka”

“So una nifukuza?”

“Toka bwana Eddy, usiendelee kunikera”

Nikamtazama Maria jinsi alivyo nuna kisha nikaufunga mlango huu na nikamsukumia kwenye kochi. Nikaivua sink taite yake pamoja cha hupi yake, nikaitanua miguu yake, nikashusha chini pensi yangu, nikamkamata jogoo wangu aliye simama kisawa sawa na nikaanza kumshuhulikia Maria, kichapo ambacho tunakiita mwana ukome. Dakika kumi na tano za mtanange huu hakika zimemfanya Maria kuchoka kisawa sawa, kiasi cha kushindwa hata kunyanyuka kwenye sofa.

“Siku nyingine usije ukaniletea dharau za kijinga kama hizi. Tumeelewana”

“Ehee hapana Eddy, ungenitoa kizazi changu”

“Ndio hivyo. Kumbuka mapema nime kukojolea nje zisije zikapita wiki hapa ukanisumbua kwamba una mtoto wangu, mama nita kunyonga”

“Eddy, mimi ni mtu mzima, ita kuwaje nikusingizie mimba ambayo sio yako”

“Wangapi wana singiziwa mimba wakiwa ni watu wazima na mavuz** yao”

Maria akatabasamu. Nikavaa nguo zangu vizuri, nikaagana naye na nikaondoka nyumbani kwake hapa. Ikanilazimu kurudi nyumbani kwangu, nikaoga tena na nguo nilizo zivaa nikaziingiza kwenye mashie ya kufulia ili mke wangu asije akahisi manikato Maria, yaliyo salia kwenye nguo yangu. Nikavaa nguo ambazo zina heshima kuingia nazo ukweni. Kwa kutimia usafiri wa bodaboda niliye toka naye kwa Maria, ndio huyu ambaye naye amenipeleka hadi nyumbani kwa wakwe zangu. Nikamlipa kiasi anacho stahili, nikasimama getini huku nikiangalia gorofa hili lenye gorofa mbili kwenda juu. Ni jumba la kifahari sana ambalo baba Cauther ana limiliki, geti likafunguliwa na mlinzi na nikaingia ndani. Cauther akatoka nje na kunipokea.

“Vipi baby mbona ume chelewa?”

“Ilinibidi nirudi nyumbani kubadilisha nguo kwa maana wakati una nipigia nilikuwa nina pensi na tisheti na nisinge weza kuja hivyo”

“Mmmm baby unge kuja hivyo hivyo kwani hapa ni ikulu”

“Sio ikulu ila ni kwa wakwe zangu”

“Haya bwana”

“Ehee hembu nipe maelezo machache ime kuwaje?”

“Ahaa baba yeye ameamua kila mtu amuandikishe urithi wake. Mimi nimepewa visima vya mafuta vile vilivyopo visiwa vya Shelisheli”

“Wooo ni vizuri”

“Yaa ila amesema kwamba urithi wake uta anza kufanya kazi kwa kila mtoto mara tu atakapo kufa. Ila kwa kipindi hichi yeye ndio musimamisizi wa mali zake zote”

“Waoo ametumia akili”

“Haya twende ndani na nimekuandalia chakula tayari”

“Wewe umesha kula?”

“Hapana, siwezi kula kama wewe upo hapa Dar es Salaam, lazima tule pamoja”

“Nashukuru mke wangu”

Moyo wangu ukajisikia vibaya sana kuona mwanamke anaye nijali na kunipenda, nime msaliti kwa mwanamke mmoja anaye nitamani tu kimapenzi.

‘Ila sisi wanaume hatudadhiliki haki ya Mungu vile’

Nilizungumza kimoyo moyo huku tukiingia ndani. Tatizo la waarabu huwa wanaishi ukoo mzima kwenye nyumba moja hivyo nikakuta seble ikiwa imejaa wazazi wa Cauther, wajomba, mama wadogo mashangazi watoto na wajukuu ndio usiseme. Nikawasalimia kwa heshima, walio itikia salamu yangu kwangu ni sawa na walio kaa kimya huku wakininyari kwa dharau yote sawa kwani siwezi kuwalazimisha wanipende. Tukaa kwenye moja ya sofa mimi na Cauther na sebleni nzima mimi ndio mtu mweusi peke yangu.

“Kijana nime kuita”

Baba mkwe alizungumza kwa sauti ya uchovu kidogo kishaa akaendelea kuzungumza.

“Binti yangu ame nieleza kwamba wewe ni nani, na kaka yake pia amenidhibistishia kwamba wewe ni nani. Je alicho kizungumza ni kweli?”

Macho ya karibia watu hamsini, yana nitazama huku ukimya ukiwa ume tawala wakisubiria jibu langu.

“Ndio”

Baba mke akafumba macho yake kwa sekunde kadhaa kisha akayafumbua na kunitazama.

“Una jua uhatari ambao una muweke binti yangu?”

“Bab…..”

Cauther alikatishwa sentensi yake kwa baba yake kumpa ishara ya kuweka kidole kimoja mdomoni mwake ikiwa ni ishara ya yeye kunyamaza na asizungumze chochote.

“Eti una fahamu uhatari ambao binti yangu una muweka?”

“Akiwa na mimi hawezi kuwa na hatari”

“Ila una muweka kwenye uhatari kutokana na hiyo kazi yako?”

“Mzee hatari ipo sehemu yoyote. Je ulifahamu kwamba utavamiwa na majambazi na kupigwa risasi na majambazi hao ni watu wa karibu sana na mwanao ulikuwa una lijua hilo?”

Baba Cauther akamtazama mwanaye mkubwa ambaye ni Salumu, kaka wa Cauther kisha akanitazama mimi usoni mwangu.

“Sikjua”

“Hivyo hakuna anaye jua kesho yake wala leo yake. Mke wangu ni dhamana yangu, akiwa ana umwa, hana furaha, hana amani, mimi ndio nina chukua majukumu yoye ya kuhakikisha kwamba ana kuwa salama. Mulimlea toka utotoni, sasa huku mbeleni mimi ndio nitakaye mlea hadi kufa kwetu”

Nilijibu kwa kujiamini huku nikimkazia macho baba mkwe.

“Unacho kizungumza una maanisha?”

“Asilimia mia moja nina maanisha na nikupe siri moja na wana familia nzima muweze kujua siri hii.”

Nikamshika Cauther mkono kiganja cha mkono wake wa kushoto.

“Endapo kuna mtu yoyote hapa duniani, ata jaribu kumdhuru, kumdharau au kumnyanyasa kivyovyote mke wangu, basi hato liona jua la kesho. Hicho ndio kiapo nilicho kiapa kwa mwenyezi Mungu. Huyu ndio furaha yangu, huyu ndio amani yangu na huyu ndio mama wa wananangu na ndio maana mulivyo kuwa muna nipiga piga mikwara mcharwa niachane naye sikudhubutu hata kumuonyesha dalili ya kuwaogopa au kukata tamaa. Niliwaheshimu kwa maana nyinyi ni wakwe zangu na Cauther ata baki kuwa mtoto wenu haha iweje.”

Cauther akanitazama na kutabasamu kwa maana nina zidi kumdhihirishia kwamba mimi ni mwanaume wa shoka na sio wanaume wa mchezo chezo ambao wakitishiwa kidogo na wakwe zao ambao wamewapita kiuchumi basi wana tetereka na wengine kuamua kuingia mitini kabisa. Ukimya wa dakika kama mbili ukatawala sebleni hapa huku kila mtu akimtazama baba mkwe na kumsikilizia ni kitu gani atakacho kizungumza. Baba mkwe akatabasamu na akaanza kupiga makofi taratibu.

“Hakika mwanangu sasa yupo mikono salama. Wewe ndio mwanaume niliye kuwa nina hitaji uweze kuoa katika familia yangu”

Maneno ya baba mkwe yakawashangaza watu wote hata mimi na mke wangu tukajawa na mshangao mkuwa sana.

”Nilihitaji kuona watoto wangu wa kike wakike wana olewa na wanaume ngang’ari na sio wanaume ambao wata oa kwa sababu ya kuhitaji kujiweka karibu na pesa zangu. Kuanzia hivi sasa tuna kupokea kama mkwe rasmi wa familia yangu karibu sana bwana Eddy”

“Nina shukuru sana mzee wangu”

Baadhi ya wana ndugu wakapiga makofi huku baadhi yao wakiwa kimya na dhairi wana onyesha kwamba hawajaridhiana na maamuzi ya baba mkwe wangu. Nikasimama na kumfwata baba mkwe pale alipo na nika kumbatiana naye kwa furaha.

“Nahitaji uilinde familia yangu na mali zangu wewe ndio mtu ninaye kuamini kuanzia hivi sasa”

Baba mkwe alininong’oneza tukiwa katika hali ya kukumbatiana. Nikajawa na mshangao kidogo kwa maana kila ninacho kiona hapa nina hisi ni kama maigizo ya filamu.

“Tuta zungumza vizuri mara baada ya kikao hichi kuisha na ita bidi pia ufunge ndoa kwa mara ya pili kwa mila zetu za kiarabu.”

“Hakuna shaka mzee”

“Basi ndoa yako ita pangwa mara moja na ndani ya wili hii basi nita watangazia matajiri wezangu wote kwamba sasa binti yangu Cauther ana olewa”

“Nakushukuru sana mzee wangu”

Nikaachiana na baba mkwe, kikao kikaishia hapa, Cauther akanikaribisha mezani na tukaanza kupata chakula.

“Bwana Shemeji”

Salum alizungumza huku akikaa kiti cha pembeni yangu.

Habari ya wewe?”

“Nina mshukuru Mungu sana. Wale washenzi, wamesha pandishwa mahakamani na kila mmoja amegongwa kifungo cha miaka thelathini jela”

“Aisee”

“Ndio shemeji. Kuseme kweli nina shukuru sana. Kumbe walikuwa wana jifanya ni rafiki zangu, wafanya biashara wezangu kumbe hawana chochote zaidi ya ujambazi ulio wajaa ndani mwao.”

“Ndio hivyo ina kupasa uwe makini na kila mtu”

“Nimejifunza shemeji yangu. Sasa hivi nipo makini tena sana”

“Safi sana”

“Alafu kaka Salu usipende kwenda kwenda huko madisko ndipo unapo kutana na watu wako wa ajabu hao”

“Now nime acha, sasa nina taka kuoa”

“Kumbe bwana Shemeji ulikuwa hujaoa?”

“Nilioa ndoa kama mbili hivi na zote zime vunjika”

“Aisee pole sana”

“Nina shukuru”

Mara baada ya kumaliza kula chakula hichi cha usiku. Baba mke akatuita kwenye moja ya bustani ya maua yenye vibanda vya kupumzikia.

“Eddy karibu sana kweye familia yangu”

“Nina shukuru sana baba yangu”

“Mwanangu nimemlea kwenye mazingira mazuri na mazingira ya dini. Pia ni mwanamke ambaye nina imani ana uwezo mkubwa sana wa kiakili katika kufanya baadhi ya mambo hususani ya kibiashara. Nina imani mukiwa pamoja mali zangu zita weza kwenda vizuri”

Baba Mkwe alizungumza huku akitutazama kwenye nyuso zetu.

“Mwanangu alinieleza mimi mwenyewe kwamba wewe ni kati ya wale watu ambao mulikuwa muna unda kikosi cha X. Kikoso cha miaka ya hivi karibuni kiliweza kupotea na kuto sikika”

“Yaa ni kweli”

“Alinionyesha na udhibitisho wa picha alizo piga ikulu akiwa na makamu wa raisi na wafanyakazi wengine.”

“Ehee kumbe ulipiga picha na makamu wa raisi?”

Nilimuuliza Cauther huku nikimtazama usoni mwake.

“Yaa ile siku ulipo kuwa una toka kumuokoa raisi, nilipiga naye picha.”

“Ahaa sija ona mimi”

“Cauther hembu kanitengenezee ile juisi yangu ya karoti ninayo ipenda”

“Usiku huu baba?”

“Ndio”

Cauther akanyanyuka na kuniacha mimi na baba mkwe. Tukamsindikiza kwa macho hadi akaingia ndani. Baba mkwe akatoa flash na kunikabidhi.

“Nime kuwa mfanya biashara mkubwa kwa miaka mingi sana na nnime weza kutengeneza pesa kwa njia halali na zisizo halali. Lilipo kuja swala la pesa nilikuwa ni mtu mwengine sana, katili na nisiye jua thamani ya uhai wa binadamu. Niliua, nilinyanyasa, nilipora na nilidhulumu hii yote ni kwa ajili ya kwamba nina hitaji niwe tajiri. Juzi nilivyo pigwa risasi, ndipo nilipo weza kugundua kwamba kuna kufa na Mungu alinipa nafasi ya kuweza kuishi tena. Eddy mwanangu, nina hitaji kumrudia Mungu wangu kwa sasa, kwenye flash hiyo kuna siri zote zinazo husiana na kundi moja ambalo nina imani huja wahi kulisikia kwenye maisha yako.”

Baba mkwe alizungumza kwa sauti ya chini kidogo huku akinitazama usoni mwangu.

“Kundi gani baba?”

“Kundi moja linalo itwa SCORPION. Mimi ni miongoni mwa wanachama wake na nimejitoa kimya kimya pasipo wao kujua chochote na endapo wata jua ni lazima wata nisaka duniani kote na kunia. Eddy hili kundi ni hatari kuliko makundi yote duniani kwa maana haliongozwi na machoka mbaya. Ila lina ongozwa na watu matajiri ambao wana nguvu ya pesa na makamu wetu wa raisi ndio kiongozi wetu. Nime kupa flash hiyo kwa ajili ya kujilinda na kujua nani ni adui kwako na nani si adui kwako kwani nilistuka sana pale Cauther alivyo nieleza kwamba wewe ni mmoja wa wanajeshi wa kundi la X. Ikiwa sisi tulifahamu wanajeshi wote wame kufa. Hivyo Eddy mwanangu, upo kwenye tanuri la moto, hakikisha una toka salama wewe na mke wako. Pia samahani kwa vifo vya marafiki zako”

Maneno ya baba mkwe yakaanza kuyafanya mapigo yangu ya moyo kuongeza kasi ya kudunda huku nikimtazama usoni mwake kwa macho yaliyo jaa hasira kali sana. Nikamuona Cauther akija eneo tulilopo huku mkononi mwake akiwa ameshika sahani yenye glasi ya juisi na kunifanya nijitahidi kuizuia hasira yangu kwani angechelewa hata dakika moja, basi baba yake leo ninge mfanya kitu ambacho asinge kaa akisahau kwenye maisha yake



“Baba nime kuwekea karafuu kama upendavyo”

Cauther alizungumza huku akimkabidhi baba yake juisi hiyo akuyo itengeneza.

“Asante sana mwanangu. Mbona hujamtengenezea na mume wako?”

“Mmmm huyu hapendi juisi za karoti. Anapendelea sana juisi ya nanasi, embe na parachichi”

Nikatabasamu ili kuificha hasira yangu inayo endelea kunitafuna ndani ya moyo wangu kwani kwa kweli baba mkwe ni mmoja wa watenda dhambi walio zulumu roho za rafiki zangu.

“Ina bidi muweze kufanya mpango wa kuniletea mjukuu kabla sijafa”

“Mmmm baba huto kufa bwana”

Cauther alilalama huku akiwa amekiegemesha kichwa chake katika bega langu la mkono wa kulia.

“Umri ume kwenda wanangu. Miaka sabini na mbili sio haba”

“Duu una umri mkubwa sana baba ila bado una nguvu zako?”

Nilimzungumza huku nikimtazama baba mkwe usoni mwake.

“Yaa katika kipindi chote nilikuwa ni mtu wa kufanya mazoezi na kujiweka mbali na pombe, sigara, kula kula hovyo hovyo. Hizo ndio zimenifanya hadi leo hii nina onekana super.”

“Alafu baba anacheza karete”

“Wacha wee”

“Yaa nina mkanda mweusi”

Baba mkwe alijigamba, laiti angejua nafsi yangu ameivuruga wala asinge nikenulia kenulia meno. Baada ya mazungumzo ya kama dakika kumi hivi, tukaaga na mke wangu na kuianza safari ya kuelekea nyumbani kwetu.

“Baby”

“Beee”

“Kwa nini uliamua kumueleza baba mimi ni nani?”

Nilimuuliza mke wangu huku nikiendesha gari mwendo wa polepole.

“Kwanza nina kuomba unisamehe mume wangu. Pili baba mimi ndio rafiki yangu kuliko mama, niliona ni vyema kumueleza yeye kwani ata weza kutuelewa na hato kuchukulia kama dereva taksi. Ona umekaribishwa nyumbani vizuri na amekupenda”

“Baada ya kunijua mimi ni nani ndio amenipenda?”

Swali langu likampa kigugumizi Cauther.

“Samahani mume wangu”

Cauther alizungumza kwa sauti ya upole sana na unyonge kwa maana amesha tambua kwamba ame kosea.

“Siku nyingine sinto hitaji umueleze mtu yoyote kwamba mimi ni nani, hata awe ni nani kwako sihitaji umuambie yoyote. Nitabaki kuwa dereva taksi hivyo hivyo sawa”

Nilizungumza kwa msisitizo na ukali kidogo.

“Sawa mume wangu nina kuomba uni samehe sana”

“Nime kusamehe”

Nikakunja kona ya kuingia mtaa ninao ishi. Taratibu nika simamisha gari mita kadhaa kutoka ilipo nyumba yangu, nikazima taa za gari huku machale yakiwa yana nicheza sana.

“Baby mbona ume simamisha gari?”

Mke wangu aliniuliza huku akiwa na wasiwasi.

“Ngoja”

Nilizungumza huku nikiuchunguza mtaa huu kwani majira ya sasa hivi ni saa nane usiku. Nikatoa simu yangu mfukoni na kuingia upande wa kamera za siri nilizo zifunga nyumbani kwangu ambapo hata mke wangu mwenyewe hajui. Nikachunguza usalama wa nje na kuwaona walinzi wakiwa wana katika katiza, nikachunguza ndani napo pia nikaona kukiwa hakuna mtu. Nikawasha gari na kuelekea hadi mlangoni, nikapiga honi moja walinzi wakanifungulia. Nikasalimiana nao kisha mimi na mke wangu tukaingia ndani.

“Kaa nyuma yangu”

Nilizungumza huku nikitangulia mbele. Tukaingia chumbani, jikoni na kila sehemu ambayo niliitilia shaka nikaipeleleza na kukuta hali ikiwa shwali.

“Baby una hisi kuna nini?”

“No kukagua usalama wa nyumba ni jambo muhimu hususani tukirudi nyakati kama hizi”

“Sawa mume wangu”

Tukaingia bafuni na kuoga kwa pamoja, uchokozi wa mke wangu ukaniashiria kwamba anahitaji kupewa haki yake na sikuhitaji kumnyima kwa kisingizio cha kuchoka. Nikaanza kumtafuna kisawa sawa hadi sote tukaridhika. Kutokana na mtanange huu, mke wangu akachoka sana na baada ya kutoka bafuni moja kwa moja akapanda kitandani na kulala. Nikamshushia neti, kisha nikafungua kabatini na nikachukua laptop yangu pamoja na earphone kisha nikakaa sebleni. Nikaichomeka flash aliyo nikabidhi baba mkwe kwenye laptop hii na nikaanza kuipekua hatua moja baada ya nyingine. Mambo niliyo yaona ni zaidi ambayo tuliyapata kwenye simu ya mkuu jeshi la waasi la DRC. Kutokana kichwa changu kina uwezo wa kuhifadhi kumbukumbu kwa kiwango kikubwa nikajitahidi kukremisha wanachama wote walipo katika kundi hili la Scorpion pamoja na maeneo wanayo patikana na kufanyia kazi kwani si mtandao wa Tanzania tu bali ni dunia nzima. Sikuishia hapo nikakremisha na akaunti nambazao za mabeki na kiwango cha pesa ambacho kila mwana chama ana ingiza kwa mwezi.

‘Kwa nini makamu wa raisi aliamua kutuua?’

Swali hili likakosa jibu kichwani mwangu. Nikajaribu kutafuta sababu ya sisi kuuwawa, ila nikaikosa kwani vikundi viwili ambavyo vime tangulia mbele yetu, kila kimoja kiliuwawa kutokana na sababu zake. Kukundi cha kwanza waliuwawa kwa kukiuka maagizo ya wakuu wao. Kikundi cha pili hivyo hivyo ila nao walifanya kazi ambayo hawakuagizwa.

‘Sisi mbona tulikuwa tuna watii na kila walicho kuwa wana kuhitaji walikuwa wana kipata?’

Niliendelea kuwaza akilini mwangu. Kuna faili moja ambalo lime fichwa sana hadi kulingundua ni baada ya kupekua pekua sana. Nikajaribu kulifungua ila nikashindwa kwa maana lina hitaji neno la siri.

“Shiti”

Nikajifikiria kwa sekunde kadhaa kisha nikaiandika jina la Cauther kwa bahati nzuri likafunguka. Nikakutana na video, nikaifungua na kumuona baba mkwe. Nikachomea earphone kwenye laptop hii kisha nikaivaa katika sikio moja,

“Utakapo kuwa una itazama video hii basi nina weza nikawa nime kufa au nikawa nipo hai ila katika hatari kubwa sana. Nilijiunga kwenye kundi la Scorpion nikiwa na umri wa miaka ishirini na tano na kipindi hicho nilikuwa na utajiri wa dola milioni tano.”

“Rafiki yangu wa karibu ambaye kwa sasa ni makamu wa raisi. Alinipa wazo la kuanzisha kikundi ambacho kita kuwa kina zalisha majasusi ambao wata kuwa wana fanya kazi katika serikali zao ila kwa mikataba maalumu kati ya wao na serikali za nchi zao. Na katika mkataba huo sisi kama Scorpion tuta kuwa tuna nufaika na malipo ya awali yatakayo kuwa yana lipwa na serikali pamoja na mashirika na sisi ndio tutakao kuwa tuna walipa majasusi hao.”

“Scorpion tume sambaa duniani kote na sisi ndio tuna mamlaka ya kumsimisha raisi yoyote tumtaka katika nchi yoyote kwa maana tuna nguvu ya pesa, nguvu ya silaha na raisi ambaye ata ingia madarakani kwa matakwa yetu na ata tusaliti au hato fwata yale tunayo yahitaji. Tunamuua kwa kutumia vikundi vikubwa na vidogo vidogo vya waasi. Vikundi hivyo tuta vidhamini kwa kuvipatia pesa na silaha pamoja na mafunzo ya kijeshi na vita weza kupambana na serikali hata iwe imara vipi ila vita shinda”

Nikashusha pumzi huku nikitazama video hii ambayo baba mkwe ameirekodi akiwa peke yake.

“Karibia asilimia stini na sita ya maraisi wote walipo duniani wapo kwa matakwa yetu. Sisi ndio tuna amua nani awe raisi na nani atoke madarakani na kwa muda gani na aweze kuishi kwa muda gani kwani tuna nguvu ya kumuua muda wowote na wakati wowote”

Nikaikumbuka kauli ya makamu wa raisi ambayo alituambia tukiwa ndani ya gari, nchini DRC ambapo alidai kwamba endapo msafara wetu uta vamiwa basi nchi kama nchi ita mtoa madarakani raisi wa DRC na ita muweka raisi ambaye ata kuwa na manufaa kwa nchi ya Tanzania.

“Wapo maraisi nane ambao Scrorpion tuna hitaji kuwatoa madarakani kwa mwaka huu. Wapo watakao kufa kwa mashambulizi ya mabomu, wapo watakao kufa kwa kupiga risasi, wapo watakao kufa kwa kutekwa, wapo watakao kufa kwa kupandizikwa virusi vya magonjwa hatari kama Ebola na kadhalika. Maraisi hawa ni kati ya wale ambao tuna endelea kuhakikisha tuna kuza utawala wa kumiliki dunia nzima kwani tume weza kuwashawishi kujiunga nasi ila wamekataa.”

“Namba moja ni raisi wa Tanzania”

Nkastuka sana na kuisimamisha kwanza hii video huku macho yakinitoka. Nikairudisha nyuma kidogo ili nisikie vizuri.

“Namba moja ni raisi wa Tanzania. Kwa sasa Tanzania ndio nchi yenye nguvu kuliko zote duniani, ina nguvu ya kifedha, kisilaha, jeshi na ina miliki visima vya kutengenezea mabomu ya nyuklia. Mabomu hatari sana duniani. Raisi mara baada ya kuingizwa madarakani na mkuu wetu ambaye kwa sasa ndio makamu wa raisi wa Tanzania. Akaanza kujawa na kiburi, maamuzi yake ni ya kwake pasipo kusikiliza maoni ya wasaidizi wake akiwemo mkuu wetu ambaye ndio makamu wa raisi.”

“Tume mpa onyo la kwanza kwa kuiteka ndege yake ili tumuonyeshe kwamba hata kama ana kiburi kiasi gani watu tuna uwezo wa kumdondosha muda na wakati tunao utaka sisi. Hatukuhitaji kumuua ila tulihitaji kumpa fundisho. Endapo ata endelea, siku ya sherehe za kuadhimisha uhuru wa nchi ya Tanzania basi ata uwawa hadharani na watu wakishuhudia”

Kauli hii ikanifanya hadi tumbo linitetemeke na kuhisi haja kubwa ikitaka kunitoka.

“Raisi namba mbili ni raisi wa China, namba tatu ni raisi wa North Korea, raisi namba nne ni wa DRC, raisi namba tano ni wa Colombia raisi namba sita raisi wa Afrika Kusini, saba raisi wa Somalia na nane ni raisi wa Kenya. Katika listi hiyo hao maraisi wote ni lazima wata kufa kila mmoja kwa kifo chake”

“Mission yetu kubwa ni kuhakikisha kwamba tuna itawala dunia kwa asilimia mia moja.”

“Sababu za kuua kikiso cha X, kikosi kilicho kuwa ni hatari sana duniani. Kikiso ambacho vijana wake watano walikuwa ni watu ambao tulianza kuwahisi kwamba ni mizimu, kwani kila wakati ambapo tulikuwa tuna panga kuwaangamiza walikuwa wana kikwepa kifo.”

Nikakaa vizuri kwenye sofa hili ili niweze kusikia.

“Vijana hawa wanne, walitupa hofu na wasiwasi wa kwamba ipo siku wana weza kutugeuka na endapo wange tugeuka japo walikuwa hawatambui wana fanya kazi na kina nani, basi wange tuangamiza ndio maana tuka wapeleka Pakistani ambapo huko walikuwa wana fanua kazi chini ya uumoja wa mataifa na huko ndipo walipo uwawa wote wanne”

‘Ina maana hawajui kwamba mimi nipo hai?’

Nilijiuliza huku nikiwaza sana, swali jengine nina waza ni kwa nini makamu wa raisi ameamua kuniacha hai ikiwa ana tambua kabisa mimi ni miongoni mwa vijana hao wa kundi la X.

‘Kuta kuwa na sababu?’

‘Ila jamaa alisema kwamba alitulengesha mikononi mwa waasi ili niuwawe, ina maana bado ana nipaka mafuta kwa mgongo wa chupa’

Niliwaza na kuazua kichwani mwangu nikakosa la kufanya, kutokana na uchovu, ikanibidi nisitishe zoezi hili la kuipekenua flash hii, nikzima laptop na kuichomoa flash na kurudi chumbani, nikaificha flash katika shelf yangu ambayo kwa mbele kuna kioo ambacho sio rahisi kwa mtu kugundua. Nikamtazama mke wangu aliye lala kihasara hasara kisha taratibu nikajilaza pembeni yake huku nikianza kumfikria na yeye kwa maana asije akawa na mpelelezi kwangu.

‘No hawezi kuwa mpelelezi, makosa ni ya baba yake na sio yeye. Nimemfanyia uchunguzi wa kutosha sana ndio maana nime muoa’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikimtazam Cauther usoni mwake. Hadi kuna pambazuka sikuweza kupata usingizi mzuri zaidi ya kujiegesha tu. Taratibu mke wangu akaanza uchokozi wake wa kimapenzi, taratibu akanikalia kiunoni mwangu huku akimkalia jogoo wangu vizuri.

“Mmmm”

Cauther aliguna kidogo kisha akaanza kuzungusha kiuno chake huku akisikilizia utamu wa penzi hili. Mtanange huu wa asubuhi asunihi ukatuchukua nusu saa nzima hadi kuumaliza.

“Asante mume wangu, sasa kiu yangu ime kwisha”

“Kweli?”

“Ndio”

“Leo kuta kuwa na sherehe ikulu hivyo baadae twende kwenye maduka tukatafute nguo nzuri”

“Kweli mume wangu?”

“Ndio”

“Waoooo mwaaaaa!!”

“Mbona ume furahi sana?”

“Mume wangu kuingia ikulu sio mchezo”

“Haahaa pachukulie kawaida, kama pele kwenu”

“Nyooo, kwetu pale hapawezi kufikia hadhi ya ikulu. Yaani siku ile nili enjoy sana”

“Basi leo uta enjoy zaidi”

“Ngoja niandae chai fasta fasta tusije tukachelewa huko madukani”

“Sawa”

Cauther akashuka kitandani na kuelekea jikoni huku akiwa amejifunga kanga moja. Nikaichukua simu yangu iliyopo pembezoni mwa kitanda. Nikatafuta namba ya raisi kisha nikaitazama kwa dakika kama tano hivi nikijishauri kupiga.

‘Sijui nimpigie huyu mzee wa watu?’

Nikaachana naye. Nikaelekea sebleni huku nikiwa na boksa tu, Cauther akaanda kifungua kifungua kinywa, tukala haraka haraka kisha tukajianda na kuelekea madukani. Tukapita katika maduka ya nguo za kike, akanunua nguo karibia kumi alizo zihitaji yeye.

“Mke wangu sasa ume nunua nguo nyingi hivyo uta zivaa leo kweli?”

“Mume wangu jamani. Kwani si kuna siku nyingine nina weza kuvaa”

“Haya”

Tukapita maduka ya nguo za kiume nikanunua suti mbili, kisha tukapita maduka ya viatu na kununua viatu tunavyo vihitaji. Mara baada ya matembezi haya, tukarudi nyumbani huku mke wangu akiwa na shahuku kubwa sana ya kwenda ikulu. Nikawaruhusu walinzi hawa kurudi ikulu kwani nimesha rudi nyumbani hivyo sina haja ya ulinzi wao tena.

“Baby”

Cauther aliniita chumbani, na nikaingia.

“Yes”

“Ahaa baba ameniambia kwamba harusi yetu ita kuwa ni ijumaa ya wiki hii”

“Ijumaa hii?”

“Ndio”

“Leo ni lini?”

“Jumenne”

“Ila ime harakishwa?”

“Usijali mume wangu, hii ni harusi kwa mila zetu za kiarabu tu, hivyo huna haja ya wewe kuingia garama nyingi”

“Kwa hiyo nita vaa suti”

“Kanzu, kilemba. Sipatipicha utakavyo pendeza mume wangu”

Mke wangu alizungumza kwa furaha sana. Saa moja usiku tukaanza safari ya kuelekea ikulu huku nikiwa nime beba vitambulisho vyangu vya kazi, tukafika ikulu ambapo kuna shamra shamra za sherehe iliyo andaliwa. Kila mtu aliye tuona nikiwa nime ongozana na mke wangu Cauther hakusita kutusifia kwamba tume pendeza kwani mke wangu ame valia gauni refu lenye mpasuo kiasi na lenye rangi ya damu ya mzee huku nami nikiwa nime valia suti iliyo nikaa vizuri mwilini mwangu na ina rangi inayo fanania na gauni la mke wangu. Maria alipo niona na mke wangu, akatufwata kwa haraka na kusimama mbele yetu na akaanza kututazama kwa macho fulani ambayo nimeweza kuyaelewa kwamba yana wivu ndani yake.

“Haki ya Mungu kaka Eddy mume pendeza sana wewe na mke wako”

Maria alizungumza kwa kumficha Cauther kilicho tokea.

“Tunashukuru. Baby huyu ana itwa Maria ni sekretari wa raisi, Maria huyu ndio wifi yako”

“Nina shukuru kumfahamu ana itwa nani?”

“Naitwa Cauther”

Cauther na Maria wakapena mikono na wakakumbatiana kidogo. Judy na Maulid nao wakafika eneo hilo nililo simama na nikasalimiana nao kwa furaha. Mlinzi mmoja wa raisi akanifwata na kuninong’oneza.

“Muangalini wifi yenu nina kuja”

Nilimuambia Judy na Maria, kisha nikaongozana na mlinzi huyu hadi katika ofisi ya raisi na kumkuta akiwa peke yake.

“Eddy funga mlango kwa ndani”

Nikafanya kama raisi alivyo niagiza. Nikakaa kwenye kiti kilichopo mbele ya meza yake, nikamsalimia raisi huku nikimtazama machoni mwake na ana onekana ni mtu mwenye hofu.

“Eddy”

Raisi aliniita kwa sauti ya upole sana.

“Naam”

“Kuna watu wana hitaji kuniua usiku wa leo hapa ikulu je uta weza kunilinda?”

Nikastuka kidogo huku nikimtazama raisi jinsi anavyo tetemeka kwa woga kiasi cha kunifanya nianze kuamini kwamba katika listi iliyo orodheshwa ya maraisi wanao paswa kuuwawa na kundi la Scrorpion basi sasa ni zamu yake kuiaga dunia.



Nikashusha pumzi nyingi huku nikimtazama muheshimiwa raisi uosni mwake.

“Ume weza kutambua ni kina nani ambao wana mpango wa kukuua usiku huu?”

“Sijajua ila moyo wangu una hisi hivyo, kwamba kuna watu wana hitaji kuniua usiku wa leo. Tana hapa hapa ikuku”

Nikakumbuka kauli ya baba mkwe aliyo jirekodi kwenye video kwamba raisi atauwawa hadharani katika sherehe za kusherekea uhuru wa nchini na sio ikulu. NIkapiga hesabu zime salia siku kumi na tano kabla ya sherehe za uhuru kufanyika.

“Mkuu”

“Naam”

“Ikulu ni sehemu salama ya wewe kuwepo. Hakuna mtu ambaye ana penda maisha yake akajaribu kufanya upuuzi wa kukuua. Nina imani tukio la kutekwa kako bado lina endelea kuitafuna akili yako muheshimiwa. Nina kuomba sana ikiwezekana uweze kuchukua likizo hata ya miezi miwili. Ukaendelee kukaa na wana saikolojia wazidi kukupa matibabu ili kidogo akili iweze kukaa vizuri kwani kwa hali hii ni hatari sana kwa afya yako”

Nilizungumza kwa upole huku nikimtazama raisi.

“Eti ehee?”

“Ndio, nina kuomba uchukue likizo mara baada ya sherehe hii kuisha”

“Na kesho je itakuwaje katika kuipokea miili ya wanajeshi walio fariki?”

“Yupo makamu wa raisi, waziri mkuu na viongozi wengine wengi. Wewe cha kufanya hakikisha kwamba leo ina kuwa ndio sherehe yako ya mwisho alafu, tafuta eneo la kwenda kujipumzisha ambapo uta kuwa wewe na walinzi wako pekee”

“Eddy simuamini mlinzi wangu yoyote zaidi yako. Nina hofu kubwa sana, mlinzi wangu mkuu niliye muamini ndio aliye nibadilika na kuwaua walinzi wengine na akatekeleza tukio la kutekwa kwangu”

Raisi alizungumza huku machozi yakimlenga lenga. Hapa ndipo nika gundua kwamba kila binadamu ana hofu ya kifo.

“Mkuu”

“Naaam”

Raisi aliitikia huku akijifuta machozi na kitambaa chake.

“Una adui yoyote ndani ya nchi hii?”

“Hapana sina?”

“Una uhakika?”

“Ndio”

“Je walio kuteka walifanya kwa kushinikiza ujitoe tu kwenye upatanishi wa migogoro ya Sudan kusini au kuna jambo jengine tofauti na hilo?”

“Sidhani nahisi ni huo mkutano ndio ume niletea mabalaa haya yote”

“Kwa nini ulimruhusu makamu wa raisi kupita katika eneo ambalo una jua kuna mapambano yanayo endelea kati ya waasi na vikosi vya usalama?”

“Lilikuwa ni wazo la makamu wa raisi nami nikaliunga mkono tu”

“Ina maana ulikuwa tayari kushuhudia walinzi wengine wakifa pamoja na makamu wa raisi?”

Raisi akakosa jibu na kukaa kimya huku akinitazama tu na kushindwa kujua ajibu kitu gani.

“Mkuu”

“Mmmm”

“Hujanijibu swali?”

“Hapana”

“Sasa kwa nini uliruhusu tutembee siku mbili kwa usafiri wa gari ikiwa una tambua kabisa nchi ya DRC haipo salama”

“X hilo lilikuwa ni wazo la makamu wa raisi na sio wazo langu.”

“Wewe na makamu wa raisi nani yupo juu?”

“Mimi?”

“Nani ni final say?”

“Mimi?”

“Kwa nini una yumba muheshimiwa. Kwa nini una waonyesha viongozi wa chini yako udhaifu. Una ongoza nchi yenye nguvu, nchi yenye pesa na yenye kutawala dunia. Kwa nini una lega lega?”

Nilizungumza kwa kufoka huku nikimkazia macho raisi. Kufoka kwangu kukamfanya raisi azidi kutetemeka hapa ndipo nikaanza kupata wasiwasi na akili yake kwani kiongozi hata akikosea hawezi kufokewa na mtu kama mimi ambaye sio hata balozi wa nyumba kumi.

“X naogopa”

“Una ogopa nini?”

“Ni….ni…..nikitoa siri”

“SIRI, Siri gani hiyo?”

Nikamshuhudia Raisi jasho likimwagika usoni mwake na moja kwa moja nikatambua kwamba hili ni jasho la woga kwani ndani ya ofisi yake kuna A/C kali hadi ambayo sio rahisi kwa mtu akaaye humu ndani kumwagikwa na jasho.

“X achana na hayo”

“Siwezi kuachana na hayo. Niliweza kuachana na vifo vya rafiki zangu walio nikiwashuhudia na nikawa sina uwezo wa kuwasaidia. Kama una hitaji nikuache na siri zako, wata kuua hao unao hisi wana taka kukuua ila kama una hitaji uwe salama. Hakikisha una nieleza kila unacho hisi kwako ni hatari. Nina hisi watu wana kusubiria ukumbini sherehe ina paswa kuanza”

Nilizungumza huku nikisimama, nikasogeza kiti nyuma, raisi akanipa ishara ya kusubiria.

“Naomba ukae Eddy”

Nikamtazama kwa sekunde kadhaa kisha nika kaa.

“Eddy”

“Naam”

“Katika utendaji wako wa kazi ume kuwa ni mwenye bidii na una ifanya kwa uaminifu pasipo kupendelea na umeitetea nchi yako kwa mambo mengi ambayo hata tukisema tukulipe hatayo fikia thamani ya yale uliyo yafanya”

“Nashukuru kwa kulielewa hilo”

“Nilitamani sana kuwaona wewe na wezako mukiwa hai hadi leo ila ndio hivyo mwenyezi Mungu aliweza kuwachukua mukiwa bado vijana wadogo wa miaka ishiri na kitu”

Raisi alizungumza kwa sauti ya upole sana na iliyo jaa busara kubwa sana.

“Eddy”

“Naam”

“Kukalia hichi kiti hapa, sio kwamba una weza kutawala kila kitu ndani ya hii nchi”

“Una maanisha nini?”

“Mimi nje nin onekana ni raisi ila ukweli ni kwamba mimi nipo kama……..”

Kabla ya raisi hajamaliza sentensi yake mlango uka gongwa.

“Muheshimiwa makamu wa raisi yupo hapa?”

Tulisikia sauti ya mlinzi, raisi akastuka sana na akaanza kufuta jasho lililopo usonimwake.

“Fungua mlango Eddy”

Raisi alizungumza kwa hofu hapa ndipo nikazidi kuelewa kwamba raisi ana ongozwa na watu walipo chini yake na yeye amekuwa kama pambo. Nikanyanyuka na kufungua mlango.

“Ohoo Eddy upo huku?”

“Ndio mzee, shikamoo”

“Marahaba nilisalimiana na mke wako, vijana wako wakaniambia kwamba uliondoka na mlinzi wa raisi”

Makamu wa raisi alizungumza huku akiwa amejawa na tabasamu pana usoni mwake.

“Yaa ni kweli”

“Muheshimiwa habari za toka mchana?”

Makamu wa raisi alimsalimia raisi huku akimpa mkono. Raisi akaupokea mkono huo huku akiwa na tabasamu ambalo nina jua ni feki na halitoki kabisa moyoni mwake.

“Nina shukuru nipo salama. Nilikuwa nina zungumza zungumza na Eddy hapa kuhusiana na ziara yenu, si unajua sija kaa naye chini toka mulipo rudi?”

Raisi alizungumza huku akijichekesha chekesha.

“Ohoo ni vizuri. Hakika Eddy akirudi kazini nina imani mambo mengi yata kwenda vizuri, mimi nime jaribu kumshawishi ila amenikatalia katu katu”

“Usijali huyu ni kijana wetu tulimtengeneza wenyewe, nina imani bado ana ile heshima ambayo alikuwa nayo”

Raisi alinisifia ikiwa hata hatuja zungumza anayo yazungumza. Nikazidi kupata picha kwamba panya ana ongoza nchi na paka ndio msaidizi.

‘Hapa hakuna raisi’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikiwatazama viongozi hawa wawili kwenye nyuso zao.

“Mkuu una subiriwa wewe tu”

“Sawa nina kuja ndugu yangu”

“Hakuna shaka”

Makamu wa raisi akatoka ndani hapa kisha akatuacha na raisi.

“Tuna weza kwendasasa”

“Upo vizuri lakini muheshimiwa?”

“Ndio”

“Basi kuwa na amani”

Raisi akashusha pumzi nyingi, akaliweka viazuri koti lake la suti kisha tukatoka ofisini hapa huku walinzi wake wanne wakimuweka katikati na mimi nime tangulia mbele. Tukafika ukumbini na mimi nikaejumuika katika meza waliyo kaa Judy, Maulid na mke wangu. Nikavuta kiti nami nika keti pembeni ya mke wangu.

“Vipo upo poa?”

Nilimgong’oneza Cauther sikioni mwake.

“Yaa nipo poa mume wangu, ndugu zako ni wachangamfu sana”

“Sawa”

Sherehe zikaanza huku muendesha shuhuli hii(mc) akitaja viongozi walio weza kuudhuri katika sherehe hii ya kuwapandishi vyeo wana usalama thelathini na moja huku mimi pekee nikiwa sipo katika listi hiyo kwani mimi bado rasimi sijarudi kazini. Ukafika muda wa kuwatunikia vyeo Maulid pamoja na Judy nao wakapata vyeti vya kupandishwa vyeo.

Baada ya walinzi hao kumalizika raisi akapewa nafasi ya kuzungumza.

“Japo tuna fahamu kwamba vijana wetu wame weza kuuwawa kule nchini DRC na makundi ya kigaidi, nipende kuwatangazia kwamba magaidi hao wame weza kuuwawa na vijaan wetu hawa ambao wame panda vyeo usiku huu”

“Ila kuna tuzo ya heshima ambayo usiku wa leo ninge penda kuweza kuitoa kwa kijana mmoja ambaye ameweza kuyatoa sadaka maisha yake kwa ajili ya nchi hii. Ameweza kuhakikisha kwamba pale wengine wanapo shindwa yeye ana fanya tena kwa njia ngumu sana.”

Judy, mke wangu na Maulid wakanitazama mimi.

“Tuzo hii ina kwenda kwa Eddy. Karibu sana”

Raisi alizungumza, watu wanao nifahamu wakaanza kupiga makofi. Nikamtazama mke wangu, kisha nikambusu kwenye lipsi zake kisha nikasimama taratibu na kuanza kuelekea jukwaani huku waandishi wa habari wakijitahidi kila mmoja kupiga picha kwa jinsi anavyo weza yeye. Nikapeana mkono na makamu wa raisi kisha akanikabidhi mdoli ulio tengenezwa kwa dhahabu huku ukiwa katika muundo wa mwanajeshi aliye shika bunduki.

“Shukrani sana muheshimiwa”

“Shukrani nawe, zungumza maneno mawili matatu”

Nikamtazama raisi kisha taratibu nikasogelea kipaza sauti, nikautazama mdolo huu ambao ni mdogo kiasi kisha nikawatazama watu wote katika ukumbi huu.

“Habari za jioni”

Watu wote wakaitikia.

“Kwanza nimshukuru Mungu kwa uhai alio nipatia. Nimshukuru mke wangu, niwashukuru watu wote ikiwemo viongozi wangu wa serikalini, makamu wa raisi baba yangu mlenzi na raisi. Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika asanteni sana”

Mara baada ya kuzungumza hivyo nikainama kidogo ikiwa ni ishara ya kutoa heshima, nikapeana mkono na raisi kisha nikatembea hadi kwenye meza kuu na kuepana mikono na viongozi walipo, kisha nikamalizia kumpa mkono makamu wa raisi na kukumbatiana naye.

“Nashukuru kwa malezi yako uliyo nipatia. Pasipo wewe, sasa hivi mimi ningekuwa ni kibaka au ningekuwa teja au kufa kabisa. Asante sana”

“Nina shukuru kwa kukumbuka hilo kijana wangu. Nina kuomba urudi kazini”

“Nakuahidi nita rudi”

“Kweli?”

“Sija wahi kukudanganya”

“Nashukuru sana”

Makamu wa raisi akajawa na furaha, nikaachiana naye kisha nikarudi kwenye meza yetu. Mke wangu akanikumbatia, hakuona aibu kunipiga busu la mdomo mbele za watu. Nikapeana mikono na Judy, Maulid, huku walinzi nilio shirikiana nao kwenye msafara wa kamaku wa raisi nchini DRC nao wakinifwata sehemu nilipo kaa na kunipongeza.

“Waoo tuzo yako nzuri sana mume wangu”

Cauther alizungumza huku akiigeuza geuza tuzo yangu na kuitazama vizuri.

“Nashukuru baby. Naona wamenifanyia suprize kwa maana hata mimi mwenyewe nilikuwa sifahamu chochote”

“Ndio raha ya suprize mume wangu laiti kama unge kuwa una fahamu hili ungesha jiandaa kiakili”

“Yaa ni kweli”

Muda wa chakua ukawadia, tukapanga mstari kama kawaida za masherehe na watu tukajipakulia vyakula na kurudi katika meza zetu na kuanza kula. Mara baada ya kumaliza kula ukafika wakati wa kucheza mziki, makamu wa raisi akamuomba mke wangu waweze kucheza na nikamkubalia mke wangu na taratibu wakaanza kucheza mziki.

“Naona una jiachia tu mwenyewe na mke wako?”

Maria alizungumza huku akikaa kwenye kiti alicho nyanyuka mke wangu.

“Sasa nisipo jiachia naye una taka nijiachie na nani?”

“Eddy mbona una zungumza kama huna moyo wewe wa kupenda. Hujali hisia zangu, au una hisi mimi sina wivu?”

Maulid na Judy mara baada ya kuona maongezi ya Maria hayawahusu wakasimama na kutuacha sisi wawili kwenye meza hii kisha wao wakelekea kucheza mziki. Nikamtazama mke wangu jinsi anavyo cheka kwa furaha sijui ana ongeleshwa nini na makamu wa raisi.

“Maria, ngoja niweke jambo moja very clear. Mimi ni mume wa mtu, nina mpenda mke wangu ndio maana nika funga naye ndoa na kumuweka ndani. Mimi na wewe ime tokea tume fanya mapenzi sawa, hatujafanya mapenzi sawa. Usije ukajaribu siku hata moja kujichanganya na ukafanya upuuzi wowote mbele ya mke wangu, labda nikuahidi jambo moja tu. Nitakuua kimya kimya pasipo mtu yoyote kujua kama nime kuua. Tumeelewana?”

Nilizungumza kwa sauti ya chini ila ya msisitizo hadi Maria akatetemeka. Akatingisha kichwa akimaanisha amenielewa.

“Nashukuru kwa kunielewa na kelele zako za wivu, mwisho ni leo sinto uniwazie akilini mwako, umenisoma?”

“Ndio, samahani”

“Twende tukacheze mziki”

Nikamshika mkono na kumnyanyua na tukajumuika na watu wengine katika kucheza mziki huku tukiwa karibu kabisa na eneo wanalo cheza mke wangu na mamaku wa raisi. Tukabadilisha wanawake mimi na makamu wa raisi na nikamchukua mke wangu na yeye akamchukua Maria.

“Vipi tuondoke?”

Nilimuuliza Cauther.

“Hapana, tusubirie sherehe iishee. Ila now ngoja nipumzike”

Tukarudi kwenye meza yetu na tukaendelea kuwatazama watu wengine wakiendelea kucheza. Muandishi wa habari mmoja wa kike pamoja na kamera mani wake wakatufwata sehemu tulipo kaa mimi na mke wake na wakaniomba waweze kunihoji.

“Sawa”

Niliakubalia na kamera mani akaelekezea kamera yake kwangu huku nikimpa ishara asiielekeze kamera hiyo kwa mke wangu na akatii.

“Umepewa tuzo ya heshima kama mtu aliye jitolea kwenye hii nchi na ume fanya kazi ngumu ambazo wengine wame shindwa, je tungependa kujua wewe ni nani kwa maana hata kwenye rekodi zetu tulivyo fwatilia hatujaona jina lako.”

Swali la muandishi huyu wa kike likanifanya nikae kimya kwa sekunde, nikatazama maiki yake ambayo ina nembo ya shirika la utangazaji la taifa.

“Mimi?”

“Ndio wewe bwana Eddy?”

Nikashusha pumzi huku nikimtazama muandishi huyu. Nafsi moja ina tamani nijitambulishe mbele za watu huku nafsi nyungine ikisita kabisa ikiohofia kuwazindua wale ambao hawajanijua na kama wapo rafiki zangu ambao ni madereva taksi wanao fwatilia tafrija hii nina imani kubwa sana wata kuwa wana shanga kuniona ikulu tena nikiwa nime pewa tuzo ya heshima kutokana na mchango wangu wa kujitolea katika taifa hili la Tanzania.



“Mimi ni mtu wa kawaida. Ni dereva taksi nina imani madereva taksi wezangu wana niona”

“Ina maana kazi yako ya udereva taksi ndio ime kufanya upewe tuzo ya heshima?”

“Ndio, kwani kuna tofauti gani msaanii legendary anapo pewa tuzo ya heshima kutokana na kazi yake?”

“Hapo sasa nime kuelewa?”

“Yaa hata kwenye udereva taksi, unapo fanya kazi ya kwako vizuri, ukaheshimu kila abiria wako unaye mpakiza kwenye taksi yako basi Mungu naye ata kunyooshea mkono wako”

“Sawa bwana Eddy tuna shukuru”

“Asante”

Nilimjibu kisiasa muandishi huyu, japo moyo wake una onekana kuto ridhika na majibu ila hakuwa na jinsi zaidi ya kuondoka eneo hiloi. Tukaa hadi mwisho sherehe ikaisha, tukaagana na viongozi kadhaa akiwemo raisi na makamu wa raisi kisha tukaondoka ikulu.

“Baby”

“Naam”

“Mbona muandishi wa habari ume wadangaya?”

“Hapakuwa na sababu ya kuwaeleza mimi ni nani. Wao waache waifanye kazi yao na sisi tufanye yetu”

“So utaendelea kuendesha taksi yako?”

“Yes maisha uliyo nikuta nayo yataendelea kama kawaida mke wangu. Sina sababu ya kubadilisha maisha kwa maana sina kazi inayo nizuia kuacha udereva wangu”

“Sawa mume wangu. Vipi uta waalika wezako kwenye harusi yetu ya kimila?”

“Hahaa naachaje kuwaalika mke wangu. Lazima wawepo”

“Nime wamiss sana mashemeji zangu. Fanya hivi, kesho nitaandaa chakula cha mchana kwa ajili ya kuwashukuru mashemeji zangu wote. Wapigie simu kesho waambie kwamba msosi kesho ni kwetu”

“Ndio maana nina kupenda mke wangu.”

Tukafika nyumbani majira ya saa tisa kasoro usiku. Kabla ya kulala nikakagua nyumba nzima kama kawaida yangu, nilipo jiridhisha, nikaingia chumbani na kujumuika na mke wangu kitandani. Asubuhi na alfajiri, nikaanza kupotea meseji kutoka kwa marafiki zangu huku wengi wakinipongeza kwa kupewa tuzo na kuwawakilisha madareva taksi, kutokana tuna chama cha madereva taksi na tuna groups katika mtandoa wa Whatsapp, nikawatumia mualiko huo na kuwaomba saa saba mchana wawe wamesha fika kwangu. Kila mmoja akaniahidi ata fika nyumbani kwangu. Cauther akaelekea sokoni kwa ajili ya manunuzi, nikawaalika Maulid na Judy ambao sasa nimesha wafanya kama wadogo zangu. Wao wakawahi kufika kabla ya wageni wengine na mke wangu mara baada ya kurudi sokoni, wakasaidiana na Judy katika kuandaa chakula.

“Aisee kaka huku maeneo ya kwenu kume tulisa sana”

Maulid alizungumza huku tukiwa tume kaa kweye eneo la kupumzikia, tukisubiria wageni kufika.

“Yaa”

“Umejenga au umepanga?”

“Nime panga miezi miwili kabla ya kufunga ndoa na mke wangu”

“Sawa sawa, kwa nini kaka usijenge?”

“Sio kama sina nyumba, ninayo ila ipo Bagamoyo. Ila kama unavyo jua mizunguko mingi sana ipo hapa Dar es Saalam”

“Hapo nime kuelewa”

“Ila mke wangu hatambui kama nina nyumba Bagamoyo kwa maana hata kunifahamu mimi ni nani amekuja kunifahamu mara baada ya kumuoa”

“Duu seme una jua kutuza siri?”

“Ndio inavyo paswa kuwa watu kama sisi, lazima siri iwe ndio silaha ya kwanza. Kufa ukiwa na siri yako moyoni.”

“Ila kwa maswala ya maendeleo sio vizuri kumficha mke?”

“No nita muambia. Una jua hawa wezetu waarabu, wengi wao huwa wana wachukulia watu weusi kama wanyama fulani. Walinidharau kweli kweli kipindi nipo na mtoto wao. Nilikuwa nimepanga kwenye geto moja hivi, kipindi nina anza mapenzi na huyu binti, alikuwa ana kuja geto hivyo hivyo. Basi kutokana na fujo fujo za wazazi wake bibie akaniongezea pesa nika panga eneo hilo ili hata wazazi wake wakija waone mtoto wao ana isha maisha mazuri”

“Sawa kaka, ila kuna binti mmoja nina mpenda ndugu yangu”

Maulid alizungumza kwa upole huku akinitazama usoni mwangu.

“So umesha mueleza hisia zako?”

“Bado kaka nina ogopa sana”

“Yaani una ogopa kutongoza mwanamke?”

“Ndio”

“Duuu, mwanajeshi mzima unaye weza kushika bunduki una shindwa kweli kutongoza. Haya huyo mwanao ulimpataje patae?”

“Yaani wee acha. Mama wa mtoto yeye ndio alinipa vishawishi hadi nika jikuta nikilala naye ila kusema ukweli sikuwahi kumtongoza ndio maana hata nilipo achana naye kwangu yalikuwa ni sawa”

“Huyo binti ana fanya kazi sehemu gani?”

“Yupo katila benki moja pale posta”

Nikatazama saa yangu ya mkononi ina onyesha ni saa tano asubuhi.

“Twende”

“Wapi??”

“Kwenye hiyo benk”

“Kaka yule manzi ni meneja wa ile benk”

“Acha woga, ngoja nikavae tisheti”

Nikanyanyuka kwenye kiti hichi, nikapita jikoni na kukuta Cauther na Judy wakiendelea kupika huku wakizungumza stori zao.

“Wacha wee kuna nukia?”

“Pishi la wifi yangu Cauther hilo”

“Hahaaa, tuna saidiana bwana wifi”

“Mmmmm nionjesheni nyama”

Mke wangu akafunua sufuria iliyo jaa nyama za kuchemsha akatoa kipande kimoja na kunilisha.

“Kuwa makini mume wangu ni chamoto hicho”

“Usijali mama. Sisi tuna toka, tuna kwenda benk pia tuta pitia vinywaji vya kuongezea kwa maana nina jua kuna watu wana kunywa wyne, wisky. Hivyo ngoja nifanya maandalizi mapema”

“Sawa mume wangu, musichelewe”

“Hakuna shida ila wageni karibia wengi si una wajua?”

“Nawajua wote, labda kuwe na dereva taksi mpya”

“Poa mke wangu”

Nikanyonyana denda na mke wangu mbele ya Judy kisha nikaingia chumbani, nikachukua kadi mbili za benki, nikabadilisha tisheti, nikapitia funguo ya gari katika meza ya sebleni kisha tukaondoka nyumbani hapa na gari langu.

“Sikia tukifika pale wewe uta niambia msichana mwenyewe ni yupi na nita jifanya ni mteja sawa”

“Sawa kaka”

“Picha yake unayo?”

“Ngoja niingie kwenye akaunti yake ya Instergram.”

Maulid akaanza kupekua pekua katika simu yake ksiha akanionyesha picha ya msichana mmoja mrefu, maji ya kunde na aliye jaaliwa umbo namba nane.

“Wooo mtoto amesimama”

“Ndio hivyo kaka, yaani nikijaribu kumueleza ukweli nahisi moyo kama una pasuka kwa hofu”

“Ila ana kujua?”

“Ndio ana nijua, alafu ni jarani yangu tu. Sema yeye ana ishi kwenye gorofa mimi nina ishi pembeni yake nyumba ya kawaida. Yaani tumetenganishwa na fensi ya ukuta tu”

“Daaa mdogo wangu mbona una kuwa mzembe. Yaani huyo ulitakiwa kumaliza siku nyingi sana, wewe remba remba kuna raisi wata mpitia shauri yako”

“Kaka ukiongea hivyo una niogopesha”

“Hahaaa wewe subiri, tuna ondoka naye huyu. Wewe niachie hiyo kazi”

Tukafika nje ya jengo la benki anayo fanyia kazi binti huyo.

“Ana itwa nani?”

“Mank”

“Ni mchaga ehee?”

“Yeea”

Tukasalimiana na maafande walio simama mlangoni hapa kisha tukaingia ndani na kuangaza angaza kila sehemu. Watu ni wengi kiasi, nikatembea hadi mapokezi na kuanza kusoma vikaratsi vya kutoa na kuweka pesa.

“Samahani dada”

“Bila samahani?”

“Meneja Manka nime mkuta?”

“Ndio yupo, uma miahadi naye?”

“No ila nina hitaji kuonana naye kama ita wezekana”

“Ngoja”

Msichana huyu wa mapokezi aliye valia shati la blue bahari na sketi ya dark bleu akanyanyua mkonga wa simu, akaminya minya batani za simu hiyo kisha akauweka mkonga wake sikioni.

“Bosi kuna mgeni wako hapa mapokezi ana hitaji kuonana na wewe”

“Ngoja nimulize”

Binti huyu akaziba simu yake sehemu ya kuzungumzia na akaniuliza jina langu.

“Nina itwa Eddy”

“Anasema ana itwa Eddy”

“Sawa mkuu”

Binti huyu akaishusha mkonga wa simu chini na kuuweka sehemu alipo kuwa ameutoa huku akinitazama usoni mwangu.

“Afande”

Dada huyu alimuita mmoja wa askari aliyomo humu ndani na akatufwata sehemu tulipo.

“Mpeleke huyu kaka ofisini kwa boss”

“Sawa”

Nikaongozana na afande huyu hadi katika gorofa inayo fwata. Akanionyesha ofisi ya boss huyo, nikagonga mlango, nikasikia sauti nyororo ikinikaribisha ndani. Nikafungua mlango, macho yangu yakagongana na macho ya Manka kwa kweli huyu dada ni mzuri sana. Suti yake ya rangi ya kijivu aliyo ivaa imezidi kumfanya kuonekana mzuri.

“Karibu sana ukae”

Manka alinikaribisha huku akionyesha moja ya kiti nami nika kaa.

“Karibu”

“Nashukuru, nina itwa Eddy”

“Eddy, sura yako sio ngeni sana, kuna sehemu nime kuona nguja nikumbuke”

Manka akakaa kimya kwa sekunde kadhaa.

“Ohoo nime kukumbuka, nimekuona kwenye gazeti hili hapa ukipewa tuzo ya heshima na raisi jana ikulu. Si ndio”

Manka alizungumza huku akinionyesha gazeti lililopo pembeni yake.

“Yaa ni mimi”

“Karibu sana mr Eddy. Mimi nina itwa Manka Tarimo ni meneja wa hii benki”

“Nashukuru kukufahamu. Nimekuja na shida mbili ila ya kwanza ndio ina muhimu mkubwa sana kuliko hiyo ya pili”

“Sawa una weza kuzungumza tu”

“Mdogo wangu ana umia, ana kosa furaha ana jisikia vibaya na anashindwa hata kufanya kazi yake kwa ajili yako”

“MIMI!!?”

Manka alihamaki huku akinikodolea macho.

“Ndio wewe. Una mtesa, una mnyanyasa una mbuguzi kwa nini lakini?”

“Mmmm labda uta kuwa umekosea mtu bwana Eddy. Au niambie huyo mdogo wako ana itwa nani?”

“Ana itwa Maulid yule jirani yako”

“Weee Maulid ni mdogo wako?”

“Ndio na ameshindwa kuvumilia hadi kuniambia. Kwa nini bwana huitaji kuja kwenye ukoo wetu eheee?”

Manka akaanza kuona aibu huku akitazama chini.

“Au mdogo wangu ana kasoro, hana vigezo vya kutembea na msichana uliye fanikiwa kama wewe na mzuri kama wewe”

“No sija sema hivyo bwana”

“Ila kwa maana ukiona mtu ana anajaribu kusema ujue moyoni amesha pata pancha huko”

“Hahaa, una ongea sana Eddy. Maulid ni kweli tuna onana naye kama jirani na uzuri nipo gorofani hivyo huwa nikitoka kupumzika huwa nina muona nje kwake, tuna salimiana, ila hatujawahi kupiga stori kabisa”

“Nina imani saa saba huwa muna kwenda lunch?”

“Yaa ila leo nina majukumu kidogo, lunch nime agiza iweze kueletwa hapa hapa ofisini kwangu”

“Fanya hivi, ikate hiyo oda. Leo nimeandaa chakula cha mchana nyumbani kwangu. Yaani tuna ondoka mguu kwa mguu hadi kwangu, uta kuwa na Maulid, mukae na muzungumze”

“Jamanai Eddy nina kazi kweli?”

Manka alilalama.

“Hata sisi tuna kazi tena ngumu kuliko hata hizi za kwenu. Ila tukipata vijinafasi tuna furahia kama hivi”

“Eddy kusema kweli ingekuwa ni amri yangu ninge toka. Ila kuna wakuu wangu wana subiria ripoti saa nane ya mchana wa leo, sasa hivi ni saa sita, nikisema nitoke kwenda kwako, ambapo sijui ni wapi hadi nirudi ita kuwa muskeli kidogo”

“Kwa hiyo ukipata ruhusa kwa wakuu wako uta weza kukubali kuondoka nasi?”

“Mmmm sidhani kama wana weza kunipa ruhusa kwa maana hii kazi ina takiwa kujadiliwa kesho mchana kwenye kikao”

“Ngoja nikurahisishie”

Nikatoa simu, nikampigia mkurugenzi wa benki hii ambaye ni rafiki yangu sema Manka halifahamu hilo.

“Fredy”

“Niambie ndugu yangu, aisee hadi kuiona simu yako basi leo kuna neema, au ndio tuzo ya heshima ndugu yangu”

“Yaani weee acha tu. Upo salama lakini?”

“Nipo vizuri ndugu yangu, maisha yana songa.”

“Sasa sikia, kwanza upo wapi?”

“Nipo Arusha, kuna semina nime kuja kuidhuria, ila bye kesho saa mbili asubuhi nita kuwa Dar es Salaam.”

“Okay nina muonba meneja wako wa benk ya hapa Posta mchana huu akale lunch kwangu?”

“Seriuosly”

“Yaa”

“Ila ndugu yangu si umeoa?”

“Ndio nime ona, ila kuna ubaya gani ndugu yangu”

“Hahaa nikajua basi una taka ukafanye mambo yetu”

“Haahahaa nimesha acha kitambo kaka. Sasa hivi ni mume wa mtu”

“Sawa hakuna shaka ndugu yangu, upo naye hapo”

“Ndio”

“Hembu mpatie simu”

Nikampatia Manka simu.

“Shikamoo mkuu”

“Sawa, nashukuru sana mkuu”

Manka akanirudishia simu.

“Sawa kaka ni wako huyo, una weza kukaa naye hadi usiku”

“Shukrani sana ndugu yangu, ukirudi Dar usinipe ndugu yangu. Au unataka tukutane kwenye matatizo pekee”

“Yaani wee acha tu. Tutawasiliana kaka”

“Nina shukuru”

Nikakata simu na kumfanya Manka kunishangaa.

“Yaani mkurugenzi wetu alivyo na ukali wote una zungumza naye hivyo, aisee kweli kila mbuyu na shetani wake”

“Ndio hivyo, mama fungansha kilicho chako, twende ukaonane na Maulid ila niahidi kitu”

“Kitu gani Eddy?”

“Utamkubalia mdogo wangu, kwa maana ukiona hadi watu nime kufwata ni kwamba ana kupenda na kukuhitaji kwenye maisha yake. Upo tayari kwa hilo?”

Manka akavuta pumzi nyingi kisha akazishusha taratibu na akatingisha kichwa akimaanisha kwamba yupo tayari juu ya hilo. Nikatabasamu kisha nikamsubiria Manka kupanga vitu vyake vizuri kisha tukatoka ofisini hapa na kumkuta Maulid sehemu ya kusubiria wateja. Manka akawaachia maagizo wafanyakazi wake kisha tukatoka nje.

“Dogo nina panda kwenye gari langu peke yangu, wewe utapanda huko”

Nilimuambia Maulid huku nikimuonyesha amfwate Manka na wakajikuta wakitazamana huku wakipata vigugumizi kwa maana wote wanavyo onekana wana pendana ila kila mmoja ana shindwa kufungua hisia zake kwa mwenzake.



Nikaingia kwenye gari langu na nikawa wa kwanza kuondoka eneo hili huku Maulid na Mank wakinifwata kwa nyuma. Nikanyanyua simu yangu na kumpigia Maulid..

“Kaka”

“Vipi umesha piga sound?

“Ahaa kaka bado mapema”

“Una zingua. Sasa sikia nyinyi tangulieni nyumbani mimi ninna pitia Mlimani hapo kununua baadhi ya vinywaji”

“Sawa kaka”

Nikakata simu kisha nikaanza safari ya Mlimani City. Haikunichukua muda kufika, nikafanya manunuzi ya vinyaji ambavyo nina fahamu marafiki zangu huwa wana penda kunya, kisha nika rudi nyumbani. Nikakuta rafiki zangu baadhi wakiwa wamesha fika nikasalimiana nao kwa furaha na kusaidiana nao kuingiza vinywaji ndani.

“Vipi baby madiko diko tayri?”

Nilizungumza huku nikimbusu Cauther mdomoni mwake.

“Tayari mume wangu. Nasubiria wageni kufika wote ili tuandae”

“Okay, mke wa Maulid yupo wapi?”

“Maulid ana mke?”

Judy aliuliza kwa mshangao.

“Ogoo kumbe hujui?”

“Acha utani kaka, haki ya Mungu sifahamu”

“Ngoja”

Nikatoka nje na kuangaza angaza, nikawaona Maulid na Manka wakiwa wamekaa kwenye moja ya eneo. Nikawafwata.

“Oya mbona huja mtambulisha mke wako kwa mawifi zake?”

Maulid akapata kiguumizi cha kunijibu. Nikamshika Manka mkono na kumnyanyua.

“Njoo nikutambulishe kwa mawifi zako”

“Jamaani shemeji mbona mapema?”

“Mapema gani, au bado hujamkubalia?”

“Ndio tuna zungumza hata bado hatujafika muafaka.”

“Muna zingua. Una mpenda dogo?”

“Ndio”

“Basi twende nikakutambulishe kwa mawifi zako”

Manka akakosa cha kuzungumza, nikaingia naye ndani na nika mtambulisha kwa Judy na Cauther, wakafurahi sana kumfahamu.

“Saidiana na wezako kutenga chakula”

Nikamuacha Manka ndani na kutoka nje kusalimiana na marafii zangu hawa ambao kwa takribani miaka mitatu nime kuwa nao katika biashara ya udereva taksi. Mke wangu akisaidana na Manka pamoja na Judy wakatuandalia chakula, kila anaye kula hasiti kutoa sifa kwa mpishi. Nikawashukuru wezangu hawa kuweza kuniandalia harusi ya ndoto yangu.

“Eddy vipi uta rudi kijiweni?”

Rafiki yangu mmoja aliniuliza huku akishushia chakula chake kwa bia.

“Kwa nini nisirudi kijiweni washakaji zangu. Pale ndio ofisini”

“Tumekuona ikulu bwana”

“Nilipotea njia ila pale ndio kwangu”

Sote tukacheka kwa furaha. Majira ya saa kumi jioni rafiki zangu hawa wakaanza kuondoka mmoja baada ya mwengine huku wali lewa chakali nikiwapa muda wa kupumzika kwa maana hawato weza kuendesha magari yao. Hadi ina timu saa sita usiku wageni wote wakawa wameondoka na nikaki na wadogo zangu hawa wapili pamoja na Manka. Tukasaidiana kusafisha nyumba na kuonyesha vyommbo.

“Jamani nina omba niweze kuondoka kesho asubuhi nia kazi ina nipasa kuiandaa na muda umesha kwenda”

Manka aliyuomba kuondoka nyumbani hapa.

“Kwa nini usiondoke na Maulid. Dogo nenda na mkeo home”

“Sawa kaka”

Maulid na Manka wakaondoka nyumbani hapa.

“Mume wangu nime choka sana”

“Pole mke wangu twende nika kulaze chumbani?”

Nikambeba Cauther na kumuingiza chumbani kwetu.

“Kwa jinsi nilivyo choka baby sina hata hamu ya kuona”

“Sawa mama lala”

Nikamtandikia vizuri kitanda kisha nikarudi sebleni na kumkuta Judy akinywa wyne taratibu. Nikaaa kwenye moja ya sofa huku tukitazama filamu ya mapigano ya kijapani inayo itwa Ninja Assasin.

“Mmm hivi hawa maninja wanacho kifanya ni kweli kaka?”

“Yaa ni kweli?”

“Mmmm”

“Ndio, mbona mimi mwenyewe ni Ninja?”

“Weee?”

“Haki ya Mungu vile. Mimi na wezangu tulipitia mafunzo hayo ya kininja. Hayo ndio mafunzo hatari kuliko mafunzo yote duniani. Mafunzo hayo yana kufanya ukinuse kifo, yaani ukifanikiwa kuyapita na ukitoka hapo wewe ni mwanaume”

Nilimuambia Judy huku nikimtazama usoni mwake.

“Aiseee kwa nini huku Tanzania yasifudishwe?”

“Huwezi kufundisha mafunzo ya kininja nje ya nchi zenye asili hiyo kwa maana ili uwe ninja ni lazima akili yako, hisia zako ziweze kupata mafunzo. Ndio maana ninja ana uwezo wa kuhisi na kunusa kama mbwa mwenye mafunzo hayo. Yaani akili zao zina tengenezwa kuwa zaidi ya binadamu wa kawaida. Ndio maana mimi hata nikiwa nime lala, mtu akikaribia tu kwenye ukuta wa nyumba yangu kama ana nia mbaya basi machale nana nicheza”

“Aisee natamani sana ninge pata mafunzo hayo”

“Iombeni serikali iweze kuwapa nafasi ya kwenda Japan. Ila ukiwa komandoo na mazoezi yako ukifika kwa hao Masamurai hufui dafu kwani wao kazi yao ni moja tu, una fundishwa kuua”

“Duuu”

“Ndio hivyo mdogo wangu”

“Kwa hiyo kaka wewe na wezako muli funzu?”

“Ndio ila kwa shida sana, ila tulifanikiwa. Ndio maana nikiwa katika oparesheni za kijeshi nina baki kuwa mimi kama mimi mwanajeshi, ila nikiwa katika kazi maalumu huusani za kuua basi nina kuwa muuaji haswa”

“Ila Maulid aliniadithia jinsi ulivyo wasambaratisha wale waasi. Yaani anavyo sema ilikuwa kama video game vile ya Call of Duty”

“Hahaaha ndio kazi hizo. Kikubwa siku nyingine muna paswa kuwa makini sana kwenye kila oparesheni munayo kwenda kwa maana maaduo ni wengi sana wanao wazingira na wengi tuna ishi nao”

“Ni kweli kaka je lile swala la Scorpion lime fikia wapi?”

“Lile nina endelea kulifanyia kazi taratibu”

“Ila kuna vigogo wengi”

“Sana, ndio maana nina kwenda kwa mwendo wa kinyonga”

Tukaaa sebleni hapa hadi alfajiri, Judy akaingia chumba cha wageni na kulala nami nikaingia chumbani kwangu. Sikupata usingizi wa kueleweka, majira ya saa mbili kasoro simu yangu ikaanza kuita. Nikaitazama kwa sekunde kadhaa kisha nika pokea kwa maana ni simu ya makamu wa raisi.

“Ndio muheshimiwa?”

“Habari ya asubuhi?”

“Salama tu, shikamoo”

“Marahaba. Njoo numbani kwamba muda huu”

“Kwema?”

“Ndio nina mazungumzo na wewe”

“Sawa”

Nikakata simu huku nikijifikiria kwa sekunde kadhaa. Nikamtazama Cauther ambaye bado yupo hoi usingizi, nikashuka kitandani, nikaingia bafuni na kuoga haraka haraka. Nikavaa suti nyeusi na shati jeusi. Nikachukua bastola mbili, huku bastola moja nikiichomeka kwenye soksi ya mguu wa kulia huku bastola nyingine nikiichomeka kiunoni kwangu, kwa nyuma.

“Baby ume amkaje?”

Mke wangu alizungumza kwa wenge la usingizi huku akinitazama jinsi ninayo iweka sawa tai yangu nyekundu shingoni mwangu.

“Salama baby. Nina kwenda nyumbani kwa makamu wa raisi ameniita. Judy amelala chumba cha wageni kule”

“Kuna kazi?”

“Sijajua ila ana dai kwamba ana mazungumzo na mimi. Hivyo tuta wasiliana”

“Sawa baby kuwa makini”

“Usijali”

Mke wangu akanibusu mdomoni mwangu kisha nikamgongea Judy na kumueleza kwamba nina kwenda nyumabni kwa makamu wa raisi. Nikaingia kwenye gari na kuondoka, nikafika nyumbani kwa makamu wa raisi na kukuta walinzi wake. Nikasalimiana nao kwa maana nina wafahamu, kisha nikaingia ndani na kumkuta makamu wa raisi sebleni.

“Karibu sana Eddy”

“Nashukuru”

“Vipi ume pata kifungua kinywa?”

“Ndio mkuu”

“Sawa, twende tukazungumze ofisini kwangu”

Nikaongozana naye hadi katika ofisi iliyopo chumbani kwake hapa.

“Aha anime kuita private kwa maana nina hitaji kuzungumza nawe kwa kina sana”

“Sawa mkuu nina kusikiliza”

Makamu wa raisi akaegemea kiti chake hichi kikubwa huku akinitazama machoni mwangu.

“Eddy”

“Naam”

“Kuna kazi nina hitaji kukupatia”

“Kazi gani?”

“Najua ni kazi ngumu na kazi haramu ila wewe ndio nina ona una weza kuifanya. Hakuna mtu mwengine ambaye ana weza kuifanya”

“Nakusikiliza”

“Kuna hii listi ya maraisi saba wana paswa kuiaga dunia”

Nikajifanya kustuka kidogo.

“Maraisi?”

“Ndio”

“Kuna mkutano wa maraisi wote duniani, utakao fanyika Berlin nchini Ujerumani. Hawa maraisi wote nane wata kuwepo katika mkutano huu ila katika mkutano huo mimi nita muwakilisha raisi wetu kwa maana siku ya mkutano huo ndio siku uhuru wa nchi yetu yaani 9 December”

Nikashusha pumzi kubwa huku nikimtazama makamu wa raisi.

“Maraisi hawa ni wale ambao tuna hitaji kunufaika na nchi zoa kwa maana bado mpango wa sisi kama Tanzania kuendelea kuitawala dunia upo pale pale”

“Muheshimiwa?”

“Ndio”

“Endapo wakifahamu kama mimi nipo nyuma ya hayo mauaji ita kuwaje?”

“Najua una skills za kuweza kufuta ushahidi na usijulikane kama ni wewe. Ulinzi utakuwa ni mkubwa sana katika hiyo siku ya mkutano nchini Ujerumani. Kwa maana viongozi wa mataifa yote duniani wata kuwa wapel”

“Nina weza kukuuliza swali jengine?”

“Ndio”

“Wana kufa kwa ajili tuna hitaji kutawala nchi zao kwenye mambo ya kiuchumi au wana kufa kama kufa wao?”

“Swali la kwanza ndio jibu”

Nikamtazama makamu wa raisi kwa macho ya kumchunguza.

“Nipatie list”

“Ila hujanijibu kama ume kubali au huujakubali?”

“Ina maana bado hujanijua hadi sasa mzee?”

“Miaka yako mitatu ya kukaa mtani bila ya kufanya kazi, ume badilika kwa silimia kadhaa, sasa hizo asimilia kadhaa bado sija zijua”

Nikatabasamu huku moyoni mwangu hasira ikinichemka mithili ya simba aliye jeruhiwa. Kwa akili yangu ya haraka haraka nikatambua kwamba makamu wa raisi ana nipatia kazi hii ili kuweza kunitia uhasama na nchi hizo ambazo ana hitaji maraisi wake wauwawe na endapo nikikamatwa basi nita kuwa ni gaidi au nisipo kamatwa nita windwa mimi na kizazi changu chote.

“Ni kweli asilimia zunngu huja zifahamu mkuu. Ila nahitaji kukuambia jambo moja nahitaji kuwa na familia bora nahitaji kuwa mume bora kwa mke wangu. Sihitaji kazi ya kuua tena, ila kama ni kufanya kazi kwa ajili ya maslahi ya nchi nita fanya ila sio kwa ajili ya maslahi ya watu fulani. Na kumbuka mikono yangu bado ina deni la vifo vya rafiki zangu wote ambao walikufa kwa ajili ya watu hao fulani. So nikiwajua nita waua mmoja baada ya mwengine kisha moyo wangu uta kuwa tayari kufanya kazi hizo”

Makamu wa raisi akanitazama kwa macho ya udadisi ila nika ficha kile anacho kitafuta kwa kunitazama machoni mwangu.

“Ina maana umesha wafahamu watu walio husika na vifo vya wezako?”

“Ndio, ni lile kundi la kigaidi, sasa nina hitaji kwenda Pakistani kiupya, nika wachinje mmoja baada ya mwengine”

“Ahaaa”

Makamu wa raisi akashusha pumzi nzito huku akinitazama usoni mwangu.

“Ndio”

“Ila lile kundi lilisambaratishwa na majeshi ya Marekani yakisaidiana na umoja wa mataifa?”

“Je kiongozi wao aliuwawa?”

“Bado haijadhibitishwa”

“Basi nita msaka na nikimpata nita muu”

“Eddy”

“Naam”

“Wewe ni mwanangu, japo sio damu yangu ila kwa jinsi nilivyo wale wewe na wezako kutoka kipindi kile hadi sasa hivi basi nyinyi ni wanangu. Nina kuomba kama baba hiyo kazi uachane nayo, hii kazi ninayo kuomba ni kazi muhimu. Ni kazi ambayo ita tufanya tuweze kuifanya nchi yetu kuimarika kiuchumi na kisilaha”

“Kuna faidia gani hapo kuwaua hao viongozi, ikiwa wapo watakaa chini na kuchagua viongozi wengine, viongozi ambao hawata kubali kuona nchi zao zina nyonywa. Hembu tutumia akili nyingine kujiendeleza katuika uchumi na silaha. Tuachane na hayo mambo ya dhuluma kwa manaa ipo siku vizazi vyetu vitakuja kulipiziwa visasi na nchi hizo ambazo leo hii tuna taka kuzulumu uhai wa viongozi wao.”

Nilizungumza kwa msisitizo na ukali kidogo huku nikimkazia macho makamu wa raisi.

“Eddy uelewi ni nini kinacho endelea”

“Nipo kwenye system kwa miaka zaidi ya kumi sasa. Nina elewa nini una maanisha. Angalizo, usije ukadhubutu kuiingiza nchi kwenye visasi na uadui na mataifa mengine kwa ajili ya faida zenu za kisiasa kwa maana endapo nchi ita kuwa na vita, hizo pesa, silaha na mambo munayo yafikiria, hayato wanufaisha wananchi zaidi ya kwamba wata kufa vifo vya kikatili na kuishi maisha ya tabu hivyo nina kuomba mkuu na muambie raisi, muachane na huu mpango wenu haramu”

Nilizungumza kwa kufoka hadi makamu wa raisi akaka kimya.

“Samahani nime tumie ukali ila acheni haya munayo yawazia hii ni nchi ambayo hamuishi peke yetu. Kuna mamilioni ya Watanzania, wana furahi kuishi kwenye nchi ya amani kama hii, ila siku mambo yakivurugika basi muta juta ni kwa nini mulikuwa viongozi”

Makamu wa raisi akashusha pumzi kidogo huku akinitazama”

“Kwa hiyo hii kazi huto ifanya?”

“Sio sinto ifanya tu. Ila sihitaji muone muna tuma mtu yoyote kuifanya hii kazi la sivyo nita muua na una jua nikizungumza nina maanisha nita muua”

Makamu wa raisi akanitazama huku uso wake ume jikunja ndita za hasira.

“Eddy huna idea una dili na mtu wa aina gani. Mimi ndio nime kutengeneza na mimi ndio nime kufanya hadi leo hii uweze kuwa hai alafu sasa hivi una niletea kiburi na kunipandishia sauti. Kumbuka mulikuwa ni vijizi tu vya mtaani na kama ningehitaji kuwaua usiku ule munge kuwa mumesha kufa. Ndio maana nime kuambia mimi ndio niliwapa nafasi ya nyinyi kuishi”

Makamu wa raisi alizungumza huku akisimama kwa hasira, nami nika simama kwa hasira na kuusogeza uso wangu karibu kabisa na uzo wake.

“Kama ulitupa nafasi ya kuishi ndivyo jinsi ulivyo tupa nafasi ya kufa. Laiti ingekuwa sio wewe leo hii wezangu wangekuwa hai. Sasa nina kupa onyo la mwisho na ukae ukijua kwamba una zungumza na mtu wa aina gani. Acha mpango wako na endapo uta dhubutu kuendelea kuufanya nina kuapia nita kuua mimi mwenyewe na sio mtu mwengine atakaye kuua. Yakumbuke maneno yangu mzee”

Nilizungumza kwa sauti nzito ambayo huwa nikizungumza nayo ujue basi tayari nimeingia kwenye ulimwengu mwengine, ulimwengu wa kufanya chochote kilichopo mbele yangu hata kuua nipo tayari kufanya hivyo pasipo kuhofia kitu cha aina yoyote.

*****


Taratibu makamu wa raisi akaka chini huku huku macho yakimtoka. Nikapiga hatua hadi mlangoni, nikasimama kwa sekunde kadhaa kisha nikamgeukia makamu wa raisi anaye nitazama kwa macho ya mshango.

“Endapo jambo lolote litatokea kwa watu wangu wa karibu, iwe wamesababishiwa ajali au wame vamiwa na kupigwa risasi. Tambua uta kuwa mtu wa kwanza katika kuhusika na sinto fwata sheria za nchi, nita chukua hatua mikononi mwangu na unajua nini kita tokea. Asubuhi njema”

Nikafungua mlango na kutoka ndania hapa huku nikiwa nimejawa na hasira. Sikumuaga hata mlinzi yoyote zaidi ya kuingia ndani ya gari langu, wakanifungulia geti na kuondoka kwa kasi. Nikiwa njiani simu yangu ikaanza kuita, nikaitamaza na kukuta ni baba mkwe, nikapungza mwendo wa gari langu kisha nikaipokea simu hii.

“Ndio baba”

“Mume amkaje huko?”

“Tuna mshukuru Mungu”

“Mbona kama haupo sawa mwanangu?”

“Nipo sawa baba”

“Sasa tuna weza kukutana asubuhi hii?”

“Ndio”

“Njoo ofisini kwangu”

“Sawa baba”

Ikanibidi kughairi safari ya kuelekea nyumbani kwangu na kuianza safari ya kuelekea Posta. Nikafika ofisini kwa baba mke na kumkuta akinisubiria. Nikasalimiana naye, nikawasalimia wauzaji wake wa kike wapatao wanne, kisha tukaingia ofisini.

“Ndio baba”

“Ahaa nimekuita kukupa taarifa kwamba mipango ya harusi yenu imesha kamilika”

“Nashukuru sana baba”

“Nina hitaji hii sherehe ifanyikie pale pale nyumbani, kuta kuwa na wageni waalikwa hata makamu wa raisi naye nime mualika. Japo najua mara baada ya kutazama video niliyo irekodi uta kuwa ume mchukia”

“Hakuna shaka”

“Ila mwanangu una onekana haupo sawa?”

“Nipo okay”

“Sawa kuna mavazi ya harusi niliyaagizia kutoka Dubai yamesha fika. Hivyo hapo lipo vazi lako na vazi la mke wako, muta kwenda kujaribisha kama yatakuwa yamewatosha ita kuwa vizuri, ila kama hayato watosha basi tuagize mengie kabla ya kesho kutwa kufika”

“Nashukuru baba”

“Sawa”

“Ila vipi hali yako?”

“Nina mshukuru Mungu kidonda kime kauka kwa nje ila kwa ndani nahisi bado maumivu kwa mbali. Hadi nina weza kuja kazini basi Mungu ni mwema”

Nikamtazama baba mkwe kwa macho ya kumdadisi hadi akajistukia.

“Vipi?”

“Umemiambia kwamba ume toka kwenye kundi la Scorpion?”

“Ndio ila wao hawafahamu kama nime toka”

“Sawa”

“Kuna nini?”

“Kama ume toka endelea kutoka ila kama upo bado toka.”

“Kuna nini Eddy”

“Kwani mmoja baada ya mwengine ana kwenda kufa”

“Eddy una jua ni hatari sana. Naomba usijihusishe kabisa na kundi hilo mwanangu”

“Sio mimi nitakao jihusisha ila wapo watakao jihusisha. Nina kuomba ukae pembeni katika hili sinto hitaji mke wangu aje kulia na kunilaumu katika hili”

Nilizungumza kwa msisitizo pasipo kumuhofia chochote baba mkwe.

“Sawa mwanangu”

Nikaagana naye na kutoka ofisini hapa huku nikiwa nimebeba begi la nguo. Nikaingia ndani ya gari langu na kurudi nyumbani kwangu. Nikamkuta Cauther na Judy wakitazama tv, nikasalimiana nao na moja kwa moja nikapitiliza chumbani kwangu. Mke wangu akanifwata huku akiwa ana buruza begi alilo nipokea.

“Baby mbona begi hili zito sana kuna nini?”

“Kuna nguo za harusi yetu. Nimetoka ofisini kwa baba”

“Waooo”

Mke wangu akajawa na furaha na kufungua begi hili, tukakuta nguo nzuri ambazo kila mmoja wetu amevutiwa nazo, tukazijaribu na zime kaa vizuri.

“Sipati picha hiyo siku ita kuwaje mume wangu kwa maana sio kwa kupendeza huko”

“Umeona ehee?”

“Ndio, vipi mbona ume beba bastola kulikuwa na kazi?”

“No ni kwa ajili ya ulinzi wangu”

Simu yangu ikaanza kuita ikiwa kitandani, mke wangu akainyanyua.

“Nani?”

“Raisi”

Cauther akanikabidhi simu yangu na kuipokea simu hiyo.

“Ndio muheshimiwa”

“Nina kuomba uweze kufika ikulu, muda huu”

“Kwema?”

“Nina mazungumzo muhimu na wewe”

“Sawa, nita fika hapa baada ya lisaa, nipo nje ya mkoa”

“Fanya hivyo”

Nikakata simu huku mke wangu akinitazama usoni mwangu.

“Hawa wazee wana taka kunizoea sasa”

“Kwa nini mume wangu”

“Kila mmoja anapo jisikia kuniita muda anao utaka yeye ana niita tu. Ndio maana niliachana na hizi kazi”

“Nenda tu kawasikilize mume wangu ndio wakuu wako wa kazi”

“Kazi kazi kazi gani, wajinga tu”

Nilizungumza kwa jazba kidogo hadi mke wangu akanishangaa.

“Baby kuna tatizo gani?”

Cauther alizungumza kwa sauti ya upole na ya kubembeleza, huku akinishika kifuni mwangu. Taratibu hasira yangu ikaanza kunishuka, huku nikishusha pumzi nyingi nyingi.

“Niambie baby nani kakuudhi”

“Ni mambo yao hawa viongozi ndio yana nichanganya”

“Mambo gani mume wangu”

“Nitakuambia pale nikiwa sawa. Vipi chai mumesha kunywa?”

“Tulikuwa tuna kusubiria wewe”

“Sawa andaa”

Tukavua nguo hizi za harusi na kuvaa nguo tulizo kuwa tume vaa. Cauther akaandaa kifungua kinywa na sote watatu tukaanza kunywa.

“Kaka upo sawa kweli?”

“Judy aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu”

“Hapana”

“Kuna nini?”

“Nita kuelezea”

“Ila mume wangu usiruhusu mawazo yakatawala hadi furaha yako ya hapa ndani. Please baby”

Mke wangu aliendelea kunibembeleza hadi nikarudi kwenye hali yangu ya kawaida. Nikamaliza kupata kifungua kinywa, nika aga na kuelekea ikulu. Nikafika ikulu, nikakabidhi bastola zangu mbili kwa walinzi wa getini kwa maana sipo kikazi. Nikaelekea ofisini kwa raisi na kumkuta akiwa na Maria.

“Sawa mkuu”

Maria alizungumza kisha akatoka ofisini hapa huku akiwa amebeba mafaili mawili mkononi mwake.

“Karibu sana Eddy”

“Nashukuru”

“Kaa tu”

Nikakati huku nikimtazama raisi usoni mwake.

“Shikamoo”

“Marahaba. Eddy nina ombi moja”

“Ombi gani?”

“Kuna binti wangu yule wa kwanza yupo nchini Ujerumani ana soma maswala yake ya master kwenye maswala ya sayansi na teknolijia. Kuna mkutano wa viongozi wa nchi zote duniani uta fanyika pale tisa December hivyo nilikuwa nina kuomba sana ikiwezekana uka mfanyia ulinzi binafsi kwani nina imani kuna watu wana weza kumteka kwa ajili ya manufa yao ili waweze kunishinikiza mimi kwenye mambo ambayo siyahitaji kama nchi iweze kufanya”

“Nime kuelewa ila una jua ni nini kina kwenda kutokea tisa December hapa nchini?”

“Mmmmm sitambui”

“Wana kwenda kuku wewe kwenye sherehe za uhuru”

Raisi macho yakamtoka, akaegemea kiti chake akafungua tai yake huku jasho likianza kumwagika taratibu usoni mwake.

“U….u…me….se…ma”

“Wana kwenda kukuua”

“Ki…na….na….nani”

“Wale ulio nieleza kwamba wana taka kukua juzi ndio hao wana taka kukuua hiyo siku.”

“Kwani Edd…..y ulisha wafahamu?”

“Ulihisi kwamba ungeniambie vile ninge kwenda kurelax, nilifanya kazi na upelelezi wangu n anime weza kutambua hilo. Sasa hapa kuna jambo nina hitaji uweze kufanya”

“Ni..ia….ambie tu Eddy”

“Nina hitaji ufanye mabadiliko, wewe ndio uende Ujerumani kwenye kikao hicho na makamu wa raisi aweze kubaki kuongoza sherehe za tisa December la sivyo una kufa mzee”

Raisi kwa hofu iliyo mtawala akajikuta akivua koti la suti yake taratibu na kubaki na shati.

“Eddy hivyo ndivyo nilivyo pangiwa siwezi kutengua?”

“Nani kakupangia, ikiwa wewe ndio mwenye kauli ya mwisho?”

“Eddy nilisha kuambia mimi hapa nipo tu, ila kuna watu wenye nguvu wana nishikilia kwa chini, na endapo watato mikono yao niliyo ikanyagia nita anguka chini”

“Sija wahi kuona raisi mjinga na mzembe kama wewe. Hadi kukalia kiti hicho sio wao walio panga, ni Mungu na Watanzania walio kuchagua wewe kwa nini una kuwa mjinga mjinga. Katika utawala wako umeshindwa kufanya uchunguzi wowote kuhusiana na vifo vya waajeshi wa X. Jana umepokea miili ya wanajeshi walio uwawa. Huelewi ni jinsi gani mambo yanavyo kwenda. Eheee?”

Nilizungumza kwa kufoka huku nikimkazia macho raisi. Ajifuta jasho lake kwa kitambaa kisha akasimama, akatembea kwa mwendo wa taraibu hadi dirishani na kutazama nje.

“Uta jisikiaje pale unapo ambiwa kwamba endapo uta kwenda kinyume na wanavyo hitaji wao wata waangamiza watu wako unao wapenda?”

Raisi alizungumza kwa sauti ya kinyonge.

“Eddy niliuwa nina kaulia na nguvu katika hii serikali. Ila toka walivyo niteka, walivyo nionyesha kwamba wana watu wao hadi ndani ya hii ikulu na wana niangalia kila ninacho fanya, Eddy nina ogopa. Nina kosa jinsi ya kufanya nielewe”

Raisi alizungumza kwa sauti ya unyonge hadi nikamuonea huruma.

“Walinzi wangu na watu wangu wote nilio kuwa nina waamini wame uwawa. Hawa nilio baki nao sasa hivi hawana nguvu kabisa Eddy. Yaani hapa nina jiona nipo uchi kabisa, tafadhali nielewe, sio kama nina penda, ila nina fanya ili kuwalinda hawa wachache nilio baki nao”

Nikasimama na kumsogelea raisi karibu yake.

“Jinsi unavyo jiweka chini ndivyo jinsi watakavyo kutawala. Jinsi unavyo jihisi mnyonge ndivyo jinsi watakavyo zidi kukugandamiza. Sasa nina hitaji unisikilize mimi, nina hitaji uniambie kila kitu unacho jua juu ya hao watu wana kufanya uwe mnyonge”

Raisi akanigeukia na kunitazama kwa macho ya huruma. Akarudi kukaa kwneye kiti chake kisha nami nikakaa kwenye kiti changu. Akafungu droo ya meza yake na akaoa faili lenye rangi nyeusi na kuniwekea juu ya meza.

“Katika hilo faili kuna maelezo ya kiongozi kundi la wale waasi walio iteka ndege yangu. Kiongozi huyo ndio anaye nipatia vitisho hivyo na ukiangalia ni kweli ana nguvu ya kufanya chochote”

Nikafungua faili hili na kulisoma kwa haraka haraka na vitu vilivyo andikwa humu ndani vyote ni upuuzi wa kumpumbaza raisi.

“Nani kafanya upelelezi huu?”

“Ni kitengo cha NSS, ndio walio fanya upelelezi huo”

“Na ndio walio kuletea huu upuuzi?”

Raisi akatoa macho huku akinishangaa.

“Hapa hakuna chochote na huyo kiongozi anavyo kutumia vitisho usiviweke akilini mwako. Fanya kama nilivyo kuambia. Wewe uta kwenda Ujerumani kwenye mkutano na makamu wa raisi ata baki haoa nchini”

“Ila Eddy…..”

“Hakuna cha ila kama una hitaji msaada wangu fanya kama nilivyo kuambia ila kama una hitaji nitoke pale mlangoni na tusijuene, fanya walivyo kuambia.”

“Ila wamesema endapo nita kwenda ujerumani wata ilipua ndege yangu?”

“Mimi nita kuwepo na hakuna wa kuilipua na nina omba kibali cha kwenda kuifanyia uchunguzi Tanzania One”

“Nime kupa kibali hicho na nina shukuru kwa kunipa ujasiri Eddy”

“Ni jukumu langu na nikiwa kama mzalendo wa nchi yangu ni lazima nifanye hivyo. Ila nahitaji uniahidi jambo moja”

“Jambo gani Eddy”

“Tukitoka Ujerumani nina hitaji uhakikishe kwamba una timua kila kiongozi nitakaye kuambia. Si kumtimua tu ila nita kuletea na udhibitisho wa makosa yake na moja kwa moja ata kwenda jela. Ume nielewa?”

“Nimelielewa Eddy nita fanya kama ulivyo hitaji”

“Dili”

Tukapeana mikono na raisi, akaniandikia kibali cha kufanya kazi sehemu yoyote na muda wowote. Akagonga muhuri kibali changu kisha nikaagana naye na kuondoka ikulu. Moja kwa moja nika elekea kwenye karakana inapo kaa ndege ya raisi, iitwayo Tanzania One. Nikafika uwanja wa ndege na kuonana na mkurugenzi mkuu anaye simamia maswala ya usalama wa ndege ya raisi. Nikamuonyesha kibali changu na akakubali kushirikiana nami katika kuifanyia uchunguzi ndege ya raisi. Tukafika katika karakana kubwa ambapo ndipo ndege ya raisi inapo kaa. Nikakuta mafundi wakifanya ukarabati wa baadhi ya maeneo.

“Ina tatizo gani hii ndege?”

“Haina tatizo mkuu, ila ni jambo la kawaida kufanyiwa service kila siku”

“Muna tambua kwamba ndege ina safari yakelekea Ujerumani?””

“Hapana mkuu, tunacho fahamu ni kwamba Tanzania Two ndio inayo ondoka”

“Basi tambueni ndege hii ndio inayo kwenda Ujerumani. Hakikisheni kwamba siku ya safari inapo fika ndege ina kuwa kwenye mazingira mazuri ya kusafiri”

Mkurugenzi macho yakamtoka kwa mshangao kwa maana kama kuna safari ya raisi tena ya mbali ni lazima wafahamishwe mwenzi mmoja kabla na sio wiki tatu kabla ya safari.

“Tume elewana?”

“Ndio mkuu”

Nikaingia ndani ya ndege hii kubwa ambayo ndio ndege kubwa kuliko ndege zote zinazo milikiwa na maraisi. Nilipo hakikisha kwamba nime fanya uchunguzi wa kutosha juu ya ndege hii, nikaondoka eneo hili na kurudi nyumbani kwangu, nikampigia simu Maulid na akafika nyumbani hapa, nikampigia simu na Willy naye akafika nyumbani kwangu kwa ajili ya mazungumzo muhimu.

“Vipi ulifanikiwa kwa Manka?”

“Ndio kaka”

“Okay nahitaji nika waonyeshe jambo moja. Mke wangu nawe jiandae”

“Tuna kwenda wapi mume wangu”

“Bagamoyo”

Tukamsubiria Cauther ajiandae kisha tukaanza safari ya kuelekea Bagamoyo. Tukafika Bagamoyo na moja kwa moja nikaelekea hadi ilipo nyumba yangu iliyopo pembezoni mwa bahari. Nyumba hii niliijenge kipindi ambacho kikundi changu cha X bado kilikuwa kina fanya kazi. Kwa juu ni nyumba ya kawaida na imezungushiwa ukuta na sio rahisi kwa mtu yoyote kuweza kuitilia mashaka. Tukashuka kwenye gari na kufunga geti.

“Karibuni ndani”

Tukaingia ndani na mke wangu akaanza kushangaa picha nyingi zilizopo ukutani zikinionyesha mimi na rafiki zangu toka tulipo kuwa vijana wadogo hadi tukawa wanajeshi.

“Kuanzia hivi sasa hapa ndipo tutakapo kuwa tuna fanyia mipango yetu. Hili ni eneo salama, eneo ambalo mimi na kikosi changu cha kwanza tulikuwa tuna fanyia mipango yetu. Njooni”

Nilizungumza huu tukiingia jikoni, nika fungua moja ya koki ya maji na taratibu eneo la sink hili la choo likaanza kufunguka hadi kukawa na usawa wa mlango, kila mmoja akashangaa, tukaingia eneo hilo la chini ambapo ndipo ilipo nyumba yenyewe. Eneo amblo hata tukivamiwa na watu wabaya hawato weza kutu pata kwani kuna milango mingine kama sita hivi ya kutokea eneo hili la chini ya hii nyumba.



“Waoooo kuzuri sana mume wangu”

Cauther alifurahi huku akitazama mandhari ya eneo hili ambalo lina seble kubwa iliyo jitosheleza kila kitu.

“Karibuni, hii ni nyumba salama. Kuna vyumba vitano huku chini. Vitatu vitakuwa vya kwenu nakimoja kitakuwa ni changu na mke wangu”

“Mkuu kwani tuna kuja kuishi hapa?”

Maulid aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.

“Tuna ingia kwenye kipindi kigumu. Kipindi cha kupambana na adui ambaye ukubwa wake ni kama Goliath na sisi ni kama Daud. Ila ina tupasa kumuangusha huyu Goliath kwa namna yoyote.”

Kila mtu akakaa kimya huku akinitazama usoni mwangu.

“Njooni”

Tukaingia kwenye moja ya ukumbia mkubwa ambao kipindi cha nyumba nilipo kuwa na wezangu ndipo tulipo kuwa tuna endeshea oparesheni zetu za kijasusi. Katika ukumbi huu kuna computer zenye uwezo wa hali ya juu katika maswala ya ufanyaji wa kazi. Kuna tv za nchi hamsini na tano zipatano ishirini na mbili, ambazo kazi yake ni kufwatilia matukio yote yanayo endelea duniani kupitia televishion.”

“Aiseee kaka sasa umenileta sehemu sahihi kabisa”

Willy alizungumza kwa furaha sana.

“Nina imani kwamba kazi sasa hapa una weza kuifanya vizuri?”

“Asilimia mia moja, hizi zote zina fanya kazi?”

“Ndio zina fanya kazi na zote ni nzuri”

Nikawasha computer zote pamoja na tv.

“Hapa ni zaidi ya commanding room ya ikulu na NSS”

“Kweli kaka”

Judy alizungumza kwa furaha.

“Njooni niwaonyeshe sehemu nyingine”

Nikawaonyesha chumba ambacho tunahifadhia silaha za kila aina pamoja na mavazi yetu ya kazi ambayo tulikuwa tuna yatumia na wezangu. Maulid akashika moja ya bunduki na kuanza kuikoki.

“Kwa kweli kaka mulikuwa mume jipanga”

“Yaa ukisikia X kweli tulikuwa ni watu hatari. Hili eneo hata serikali hawaitambui na kwa juu una ona ni nyumba ya kawaida kabisa.”

“Nani aliwatengenezea hivi kaka?”

Judy ailiuliza.

“Kuna rafiki zetu wakandarasi wa nchini Japani ndio walitutengenezea hivi kwa siri na hili eneo lipo chini sana kiasi kwamba hata mtu akichimba msingi wa nyumba yake na kujenga hawezi kutufikia.”

“Aiisee hii kiboko”

“Hii nyumba ime tengenezwa mahususi kwa ajili ya ulinzi binafsi, hivyo tukiwa katika mapambano yetu tutaanzia kuyapanga humu ndani na kuelekea nje”

“Ila mume wangu kwa hiyo kule tuta hama?”

“Kwa muda, uta kaa hapa hadi pale nitakapo kuambia hali ni salama”

“Mmmm baby jumba lote hili?”

“Ndio mke wangu”

“Nita ogopa ni bora niwe ninakaa nyumbani”

“Shemeji, hatari ambayo tuna iendea sio ya kawaida”

Maulid alizungumza huku akimtazama Cauther usoni mwake.

“Muna zungumzia hatari gani?”

Cauther aliutuuliza huku akitutazama kwa macho yaliyo jaa udadisi.

“Tuta ongea mke wangu baadae”

“Sawa”

Mara baada ya kuwaonyesha kila eneo la nyumba hii, tukakaa sebleni kwa ajili ya mazungumzo ya kina.

“Mke wangu tuna kuhusisha kwenye mambo nyeti ya kiserikali ambayo huja paswa kuyasikia wala kuyaelewa. Ila nina kuomba sana uwe na kifua, uwe ni mtunza siri na hata siku ikitokea kitu chochote nina kuomba usiweze kuzungumza lolote. Umenielewa?”

“Nime kuelewa mume wangu”

“Wifi tuna maanisha”

“Nina waelewa wifi yangu.”

“Leo nilikwenda kwa makamu wa raisi asubuhi na mapema sana alinipigia simu kwa ajili ya mazungumzo. Nilipo fika aliweza kunieleza juu ya mkutano mkuu wa viongozi wote wa dunia, I mean maraisi wote duniani. Kikao hicho kitafanyika Berlin nchini Ujerumani, katika siku ya tisa December ambapo nchini Tanzania ita kuwa ni siku ya kusherekea uhuru”

Nikaa kimya huku nikiwatazama watu wote sebleni hapa.

“Kuna listi ya maraisi saba kama alivyo niambia yeye. Ila ni ya maraisi nane wana paswa kuuwawa katika mkutano huo na akanipa jukumu hilo”

“Mungu wangu!!”

Cauther aliamaki huku akinitazama kwa mshangao.

“Nilicho weza kukigundua kwa makamu wa raisi ni kuhitaji kunipoteza, alihitaji kuniweka katika mtego ambao nikikamatwa ni lazima nita uwawa kwa maana kuna nchi ambazo hazina msamaha kwenye makosa kama hayo”

“Mmmmm”

Judy aliguna.

“Nilikataa kazi hiyo na nika mpa onyo kali kwamba aachane kabisa na mpango huo kwa maana kama ni nchi yetu ina hitaji kuendelea kuwa na nguvu ni lazima ijitengenezee uhakika wa kuweza kulinda maliasili zake na kuziendeleza na sio kwenda kwenye nchi nyingine kupora maliasili zao ili sisi tuzidi kwenda juu kiuchumi. Sijui kama muna nielewa?”

“Ndio tuna kuelewa”

“Mume wangu nina weza kukuuliza swali?”

“Uliza tu”

“Ina maana makamu wa raisi yeye ndio ana ratibu mipango ya kuwaua hao maraisi?”

“Ndio”

“Mungu wangu kumbe yule mzee ni mshenzi sana ehee?”

“Ndio maana nime kuambia kwamba tuna kuhusisha kwenye mambo nyeti, mambo ambayo ni siri ya nchi. Hivyo sinto hitaji kuyasikia kwa mtu yoyote”

“Nakuelewa mume wangu”

“Mkuu listi hiyo ni ya maraisi wa nchi gani?”

“Nina kuja huko ila katika listi ya maraisi hao saba, yupo mmoja ambaye alijifanya kumtoa ili kuonekana kwamba hayupo kwenye listi hiyo ila mimi nina mfahamu ni nani ambaye pia wana hitaji kumuua”

“Ni nani huyo”

“Maraisi ambao wame pangu kuwauwa Beriln ni wa nchi hizi. Raisi wa China, North Korea, DRC, Colombia, Afrika Kusini, Somalia na Kenya. Hiyo ndio listi ya maraisi saba”

“Raisi wa nane ni nani?”

Willy aliuliza huku akiwa na shahuku kubwa sana ya kuhitaji kufahamu.

“Namba nane na ambaye ana paswa kuwa ni namba moja kwenye hiyo listi ni raisi wetu wa Tanzania”

Kila mtu akastuka huku akiwa amejawa na mshangao”

“H…u….u…..yu raisi wetu?”

Cauther aliuliza.

“Ndio”

“Juzi usiku kwenye sherehe pale ikulu mlinzi wake aliniita na nikaelekea ofisini kwake?”

“Ndio”

“Nilikwenda ofisini kwake na usiku ule aliniambia kwamba kuna watu wana hitaji kumua katika ile sherehe”

“Weee ni kina nani?”

Maulid alihoji.

“Hawajui ila ana tumia vitisho ambavyo vina mfanya ashindwe kuwa na mamlaka ya kuongoza nchi”

“Duu!!”

“Isitoshe tukio la kutekwa kwake raisi ndio limezidi kumfanya awe out of power. Kwa sasa ni muoga, maamuzi yote yana fanywa na makamu wa raisi na hata kwenye hicho kikao alipanga aende makamu wa raisi alafu yeye ashiriki katika sherehe za siku ya uhuru ambapo katika siku hiyo ndipo yeye atakapo uwawa”

“Ohoo Mungu wangu”

Judy alizungumza kwa sauti iliyo jaa huzuni.

“Hadi ninavyo zungumza hivi sasa ni kwamba raisi ameishiwa nguvu. Raisi hana mamlaka tena kuna watu nyuma yake ndio wana iongoza hii nchi. Akilini mwake ana jua ni wale watu walio mteka ndio wana mpa vitisho na wana mueleza kwamba ndani ya ikulu wame weka watu wao ambao wana mfwatilia hatua hadi hatua kiasi cha kumfanya ashindwe kuwa katika misimamo yake”

“Hao watu ni kina nani?”

Cauther aliuliza.

“Ni makamu wa raisi na watu wake”

“Mmmm hayo mambo ni mazito jamani?”

“Ndio maana nilikuambia mke wangu una paswa kuwa na kifua.”

“Mkuu tuna fanyaje kuyazuia hayo?”

Maulid aliuliza.

“Nilicho mueleza raisi ni kwamba yeye ndio ana paswa kwenda nchini Ujerumani na makamu wa raisi ndio ata kuwa kiongozi wa siku ya uhuru. Mission yetu sisi watatu tuna kwenda nchini Ujerumani kuhakikisha kwamba tuna mlinda raisi. Willy uta baki hapa pamoja na mke wangu, kila kitu kinacho husiana na kazi yako kina patikana hapa, jukumu lako wewe ni kuhakikisha kwamba uta tupatia kila iana ya information ambayo tuta kuwa tuna ihitaji tukiwa nchini Ujerumani”

“Nimekuelewa kaka?”

“Mke wangu, Willy ata kuwa ana kulinda hapa. Kwenye hii nyuma kila eneo tume funga kamera ambazo kila kitu ambacho kitakuwa kina endelea ndani humu, hata tukiwa nchini Ujerumani tuta kiona”

“Duuu”

“Mbona una guna mke wangu?”

“Kwa hiyo kamera zipo hadi mavyumbani?”

“Ndio, hii ni kuhakikisha kwamba usalama una kuwa kila sehemu”

“Mkuu Ujerumani tuna kwenda lini?”

“Next week.”

“Sawa sawa”

Tukaa nyumbani hapa hadi majira ya saa nne usiku kisha tukaondoka na kurudi jijini Dar es Salaam. Judy, Maulid na Willy wakaelekea nyumbani kwao nami mimi na mke wangu tukaelekea nyumbani kwangu.

“Ila mume wangu wewe ni msiri sana”

“Kwa nini?”

“Ile nyumba yote kule ulikuwa huja nijaniamia hadi leo ndio umenionyesha pamoja na vijana wako”

“Samahani mke wangu, kuna wakati mambo mengine ina bidi yawe hivi kwa maana sikupanga kurudi kazini ila kutokana na uhitaji ninao uona sasa hivi kwenye nchi yetu ni lazima iwe hivi”

“Ila mume wangu ina bidi uwe makini sana”

“Nipo makini zaidi ya unavyo fikiria”

“Nina kupenda sana Eddy”

“Nina kupenda pia mke wangu”

Mke wangu akaka mapajani mwangu na kunikumbatia kwa hisia kali za kimapenzi.

“Leo nipo pd mume wangu”

Mke wangu alizungumza mara baada ya kumuona nina mtomasa katika maeneo ambayo yana mpandisha hisia za mapenzi.

“Ohoo pole mke wangu”

“Nashukuru, nahisi ime wahi kuja, kutokana ile mikiki mikiki ya jana”

“Ni kweli, ila tumbo haliumi?”

“No haliumi, ila asubuhi ilitoka nyingi kiasi, ila toka tumekwenda Bogamoyo, nime jisikia ikitoka kidogo tu”

“Pole mpenzi wangu”

“Nashukuru mume wangu”

Tukapata chakula cha usiku kisha tukaingia ndani kulala. Asubuhi nikwa mtu wa kwanza kuamka, nikawapigia Maulid, Judy na Willy kuwaulizia hali zao na kila mmoja kanijulisha ame amka salama. Baba mke akanipigia simu

“Shikamoo baba”

“Marahaba, mume amkaje huko kwenu”

“Tupo salama tu baba”

“Ok leo muna ratiba gani?”

“Hatuna mzee”

“Basi nina waomba muweze kuja nyumbani mchana ili tupange taratibu nyingine za ndoa, si una jua siku zimesha kwisha?”

“Sawa baba”

Nikakata simu huku nikimtazama Cauther anaye jivuta vuta kitandani. Taratubu akanipiga busu la mdomoni kisha akakilaza kichwa chake kifuani mwangu.

“Ume amkaje mume wangu?”

“Nimeamka poa mke wangu vipi wewe?”

“Nipo safi”

“Baba amesema mchana twende kwake”

“Leo”

“Ndio”

“Sawa baby”

Kutokana na uchovu alio nao mke wangu. Nikafanya kazi zote za hapa nyumbani, kisha nikamuandalia kifungua kinywa. Kwa pamoja tukapata kifungua kinywa hichi. Mchana ukawadia kisha tukaelekea nyumbanii kwa wakwe zangu na tuka pokelewa vizuri na wakwe zangu hadi nikashangaa. Maandalizi ya harusi yetu yanazidi kupamba moto. Nikatambulishwa kwa wazee wazee wa kiarabu walio toka Oman kuja kwa ajili ya sherehe hii.

“Hongera sana kwa kuwa na binti yetu”

“Nashukuru sana”

Mara baada ya utambulisho nikasogea pembeni na baba mkwe kwa ajili ya kuzungumza huku Cauther akiendelea kusalimiaa na ndugu zake alio potezana nao kwa kipindi kirefu.

“Vipi mwanangu, uliweza kuifanyia kazi ile flash?”

“Ndio”

“Umefanikiwa kujua kila kilicho ndani”

“Ume fanya maamuzi gani?”

“Bado mzee”

“Kuna hatari ambayo ina kuja mbele yangu”

“Hatari gani mzee?”

“Sifahamu ila nina ona kuna hatari hiyo Eddy mwanangu.”

“Kwani walisha kustukia kama ume ondoka kwenye umoja wao?”

“Sijui, ila huu ukaribu wangu na wewe wana weza kuuchukulia kivingine ila ngoja tuone”

“Je ulinzi ni wa kutosha?”

“Ndio ulinzi ni mkali sana na nimesha ajiri walinzi wengine zaidi kuhakikisha siku ya harusi hakuna jambo baya ambalo lina kwenda kutokea.”

“Sawa, je mpamgo wa kuuwawa kwa raisi bado upo?”

“Ndio na nina habari mbaya”

“Habari gani?”

“Raisi ame panga kwenda yeye mwenyewe Ujerumani katika kikao hicho na kilicho pangwa ni kwamba ata kwenda kuuwawa huko huko Ujerumani yeye na wale wote ambao wana kwenda huko”

Nikashusha pumzi huku nikimtazama baba mkwe usoni mwake.

“Hilo limepangwa lini?

“Jana usiku pia wana dai hii ita saidia kwa makamu wa raisi kuweza kuapishwa na kuwa raisi wa hii nchi hapo ndipo unyama wote wa nchi ambazo ana tamaa nazo ana kwenda kuufanya”

“Vipi hamjanizungumzia mimi?”

“Hapana hujazungumziwa kwani makamu wa raisi kipindi cha nyuma tulipo muuliza kuhusiana na wewe alidai kwamba uweze kuachwa huru kwani ipo siku tuta kutumia”

“Ahaa. Je wauaji wamesha andaliwa?”

“Ndio wame andaliwa wauaji maalumu kumi na mbili kutoka nchini Japan na hao wote ni maninja na wata ingia nchini Ujerumani wiki hii kuhakikisha wana fwatilia ni wapi raisi wa Tanzania ata fikia na wata hitaji kufahamu list ya walinzi wote watakao mlinda na uwezo wao ili iwe ni kazi raisi sana kwa wao kuweza kuwasambaratisha.”

Data alizo nipatia baba mkwe zikanifanya nitabasamu moyoni mwangu kimya kimya huku nikianza kupanga mbinu na mipango ya haraka ya kuhakikisha kwamba raisi ana kwenda Ujerumani salama na ana rudi nchini Tanzania salama pasipo wauaji hao kumtia mikononi mwao.



“Sawa ikiwezekana nita omba uweze kunipatia picha za wauaji hao?”

“Bado hazijatolewa ila kipo kikundi cha maninja hao walio tumwa kwa ajili ya kazi hiyo”

“Sawa”

“Ila Eddy mwanangu kuwa makini sana kwa maana hakuna usalama wowote”

“Usijali mzee”

Baba mkwe akaitwa kwa ishara na mke wake na akaniacha huku nikiwaza nini cha kufanya. Nikamtumia ujumbe mfupi Cauther na kumuomba atoke nje.

“Vipi mume wangu”

“Nahitaji kwenda ikulu mara moja”

“Kufanya nini?”

“Kuna ishu nina hitaji kwenda kuzungumza na raisi”

“Sawa, vipi ume muaga baba?”

“Hapana uta niagia ila usimuambie ni wapi ninapo kwenda”

“Mmm sawa baby”

Nikaingia kwenye gari langu na kuondoka nyumbani hapa. Nikampigia raisi na kumtaarifu kwamba nina mfwata ikuku, na akanikaribisha. Baada ya nusu saa nikafika ikulu na moja kwa moja nikaingia ofisini kwa raisi.

“Shikamoo mzee”

“Marahaba Eddy, leo ume nipigia simu kuna nini ulicho kigundua huko?”

“Nisikilize kwa umakini sana. Nina hitaji uweze kumpa maagizo jenerali wa jeshi kwamba mipaka ya nchi iimarishwe, kwa asilimia mia moja, kama kulikuwa kuna kulege lage basi wahakikishe kwamba hakuna kulegelega tena”

“Kwa nini Eddy”

“Ukiondoka nchini ina bidi nchi iwe katika ulinzi dhabiti. Hilo tuachane nalo ila linilo nileta hapa nina hitaji atengenezwe raisi mwengine wa bandia ambaye uta jumuika naye kwenye dhiara ya kuelekea nchini Ujerumani”

“Atengenezwe kivipi Eddy?”

“Atafutwe mlinzi, atengenezewe umbo kama lako, sura yako na yeye ndio ata simama kama raisi ambaye ata pokelewa nchini Ujerumani na kuelekea hotelini alafu wewe kama wewe uta baki ndani ya ndege hadi pale nitakapo kuruhusu kwamba utoke ndani ya ndege”

“Sawa, nimekuelewa Eddy. Ila niambie kuna sababu gani ya kufanya hivyo?”

“Hivi una hisi wanao iwinda roho yako wame sinzia. Wana fanya kazi usiku na mchana kuhakikisha kwamba wana kuondoa na si wewe peke yako kuna maraisi saba ambao nao wana paswa kuuwawa katika siku hiyo ya kikao chenu”

“Ohoo Mungu wangu. Eddy au nisiende?”

“Una kwenda”

“Sa….a…..sa…”

“Mzee hakuna cha sa…sa….sa….Lazima uende na huyo raisi feki nita mjua mimi na vijana wangu. Walinzi utako ingia ndao ndani ya ndege pia hawato tambua hilo. Ume nielewa?”

“Sawa nime kuelewa. Niambie nikusaidie nini na nini?”

“Nahitaji kwa sasa kwenda kwenye kambi ya jeshi ya Kigamboni. Kuna rafiki yangu pale nina hitaji kumpa kazi hiyo ya kuwa raisi feki”

“Sawa, nakushukuru sana Eddy”

“Asante. Ila kuanzi hivi sasa, ukitaka kutoka kwenda mahala popote nje ya hii ikulu. Hakikisha unanitaarifu”

“Nime kuelewa”

“Ni hayo nina ondoka”

“Je mwanangu”

“Mwanao tuta shuhulika naye”

“Asante”

Nikatoka ofisini hapa na kukutana na Maria kwenye kordo ya kuelekea kwenye ofisi ya raisi.

“Eddy tuna weza kuzungumza?”

“Sasa hivi?”

“Ndio”

Nikatazama saa yangu ya mkononi kisha nikamtazama usoni mwake.

“Tuna dakika tano, zikidizi kumi”

“Nashukuru”

Tukaingia ofisini kwake na akafunga mlango.

“Eddy, natambua kwamba una mke na una mpenda sana mke wako. Ila nina kuomba unijali japo na mimi. Toka majizu nilikuwa nina jifikiria sana mambo uliyo niambia kipindi ambacho tulikuwa tuna cheza mziki. Niliogopa”

“Maria, akili yangu kwa sasa ina wazia safari ya raisi kuelekea nchini Ujerumani. Hayo mambo yamapenzi, tuyaweke pembeni kidogo”

“Na wewe una kwenda nchini Ujerumani?”

“Ndio”

“Ohoo basi nita pata muda mzuri wa kuzungumza nawe tukiwa angani”

“Poa. Baadae”

“Eddy jamani hata busu”

Maria alizungumza huku akinishika mkono wangu wa kulia. Nikamtazama kwa sekunde kadhaa kisha nikambusu shavuni na kutoka ofisini hapa. Nikaingia kwenye gari na kuelekea katika kambi ya jeshi iliyopo Kigamboni. Nikafika getini na nikatoa kibali changu alicho niandikia raisi cha kuweza kuingia sehemu yoyote ambayo ni mali ya serikali ya nchi hii. Nikaruhusiwa kuingia, nikasimamisha gari langu kwenye maegesho, kisha nikaelekea katika ofisi ya mkuu wa kambi hii. Nikampigia saluti kwa maana nina mfahamu mzee huyu na yeye ana nifahamu vizuri sana.

“Eddy ni muda mrefu sana ume pita hatujaonana”

“Ni kweli mkuu, mara ya mwisho kuonana ilikuwa ni kipindi kile tuna jiandaa kwenda kufanya kazi UN?”

“Yaa ulikua bado kijana, ila sasa naona sura imesha anza kukomaa”

“Ni kweli ni majukumu yameongezeka”

“Ume rudi kazini kwa maani nilisikia ume acha kazi?”

“Nipo katikati, mguu mmoja ndani mguu mwengine nje”

“Kwa nini?”

“Bado nina tazama upepo. Nimekuja kumfwata lutenat John Msuya”

“Ohoo yupo ngoja nimpigie simu”

“Nisikusumbe, nielekeze kwa sasa ana weza kuwa wapi?”

“Mmmm mchana huu yupo kwenye uwanja wa mafunzo”

“Nashukuru mkuu kwa heri”

“Asante nawe kwa kuja. Alafu kabala ya kuondoka nina omba upite hapa”

“Sawa”

Nikatoka ofisini hapa, na kila wanajeshi ninao kutana nao wana nipigia saluti kwani nina cheo kuwapita wao. Nikafika uwanja wa mazoezi na kumkuta Lutenat akiwa na vijana wa mwaka wa kwanza akiwapigisha maoezi.

“What the fuc*** Eddy ni wewe?”

“Ni mimi ndugu yangu”

Tukakumbatiana kwa furaha kubwa sana kwa maana ni kipindi kirefu hatujaonana.

“Naona maisha ya ikulu ni mazuri?”

“Sifanyi kazi ikulu ndugu yangu?”

“Weee si nilikuona kwenye tv, nikahisi nime kufananisha?”

“Ni mimi ndugu ila sipo ikulu”

“Ila pole sana ndugu yangu. Washkaji zetu ndio hivyo wame ondoka bado mapema sana”

“Nashukuru na nimesha poa. Ndugu yangu nina omba msaada wako”

“Msaada gani?”

Ikatubidi tutafute sehemu ya kukaa kwa jaili ya kuzungumza.

“Nina hitaji uweze kuvaa umbo la plastiki la raisi wetu katika safari ya kuelekea nchini Ujerumani kwa maana nina jua una uwezo wa kuigiza sauti za mtu yoyote”

“Ahaa kwani raisi yeye ana nini?”

“Kuna watu wana muwinda wamuue. Ila nina nahitaji ukiwa katika mwili na sura hiyo ya bandia, ita kuwa ni rahisi sana kuweza kumkamata adui yetu”

“Hiyo ni golden Chance Eddy siwezi kuikataa japo kuwa ni hatari sana”

“Najua ni hatari kuliko unavyo fikiria, ila nina imani una weza kujilinda”

“Asilimia mia moja nipo fiti na ni siku nyingi sija pata mission za kutoka nje, kidogo hii ita nipatia ujuzi”

“Basi nashukuru. Kesho saa mbili asubuhi nita kupigia simu na kukuambia ni wapi tukutane, ina bidi uweze kujua key point za raisi. Kutembea kwake, kuongea kwake, kutazama kwake, body stracture yake ipo vipi. Kwa kufanya hivyo adui yetu tutakuwa tume mpiga dole la kati”

“Haahaa kaka ujaacha matusi tu?”

“Fala wewe, mwenyewe hapa si ume nipokea kwa matusi, nina achaje kwa mfuno ikiwa kazi zetu hizi bila kutukana hatuwezi kwenda sawa”

“Ila ni kweli, ni sawa na mboga ikakosa chumvi”

“Kumbe ume nisoma. Ndugu yangu nina kutegeme katika hilo”

“Siwezi kukuangusha. Ila kwa nini ume weza kunifikiria mimi nipate kazi hiyo?”

“Futi zako ni sawa na futi za raisi kiurefu. Kitakacho fanyika ni hiyo plastic body ya raisi kuongezewa mambo mengine ikiwemo kitambi chake kila cha uzushi”

“Poa poa kaka ila hongera kwa kuoa”

“Nina shukuru ndugu yangu”

“Naona umepata mtoto muarabu”

“Kama kawaida ndugu yangu. Nataka kuchanganya changanya rangi”

“Hahaa poa poa kaka”

Tukabadilishana anamba za simu na Msuya kisha nikaagana naye na nikarudi ofisini kwa mkuu wa kambi.

“Ehee Eddy, nililikuwa na wazo moja hivi sijui kama lita saidia”

“Wazo gani?”

“Una onaje tuka kuandalia siku moja ambayo uta kuwa una kuja kuwapa mazoezi hawa vijana kwa maana kuna vitu ambavyo wewe ulifundishwa miaka ile ila hawa vijana wana kosa”

“Nita lifikiria na kukupatia jibu”

“Nitafurahi zaidi itakapo kuwa ni jibu zuri”

“Nashukuru mkuu”

Nikaondoka kambini hapa na kurudi nyumbani kwa baba mkwe.

“Mume wangu, chakula tayari”

Nikajumuika na familia nzima na kupata chakula hichi kilicho andaliwa vizuri.

“Kijana una jishuhulisha na nini?”

Babu yake Cauther amabye ni baba wa baba mkwe aliniuliza huku tukiendelea kula.

“Mimi ni mfanya biashara”

“Waoo una shuhulika na biashara gani?”

“Baba tuna kula”

Baba mkwe alimuomba mzee huyo ambaye umri wake una onekana kwenda sana.

“No nataka kujua, ni mkwe wangu na ameingia kwenye familia ya wafanya biashara hivyo ni lazima nifahamu mjukuu wangu ni wapi anapo kwenda”

Watu wote wakaka kimya huku wakisubiria jibu langu.

“Nina kampuni ya usafirishaji wa magari.Nina chukua magari kutoka nchini Japan, Marekani, Uingereza na South Afrika na nina yauza nchini hapa”

“Ni magari Used?”

“Yapo mapya na Used”

“Ahaa nina jua una pesa”

“Kiasi chake”

“Cauther”

“Abee babu”

“Una mpenda mwenzio?”

“Ndio babu”

“Ina bidi mupendane. Muna jua siri kubwa ya mimi kukaa kwa muda mrefu na bibi yenu ilikuw ani uvumilivu, ukweli na kusameheana. Mukiviweza hivyo vitu, haki ya Mungu nina waapia, muta dumu na kufika maisha kama haya yetu”

“Nashukuru sana babu”

Nilizungumza kwa sauti ya upole kwa maana bado watu wana endelea kula. Nikamaliza kula na baba mkwe akanieleza kwamba Cauther ina bidi kwa siku hizi chache zilizo salia kabla ya ndoa yetu ina bidi aweze kubaki hapa nyumbani kwao.

“Hakuna shaka mzee”

“Nilihisi labda una weza kugadhifika?”

“No, mimi sio mtu wa hivyo mzee wangu”

“Nashukuru sana kwa mwanangu kupata mtu muelea.”

“Usijali”

Baba mke akaondoka katika eneo hili la kupumzikia na Cauther akanifwata.

“Vipi baba amekuambia kwmaba nina bidi nibaki?”

“Yaaa ame niambia mke wangu”

“Nakuonea huruma uta kuwa mwenyewe nyumbani”

“Usijali mke wangu, si keso kutwa tu ndio tuna kula ubweche kwa mara ya pili”

“Yaani mume wangu, sikutarajia kama mambo yanaweza kuwa hivi. Vile vitisho walivyo kuwa wana kupiga kwa mara ya kwanza….Mmmmm”

“Ndio hivyo watu wana badilika mke wangu. Vipi kwanza period?”

“Ina toka kwa mbali?”

“Maumivu hakuna?”

“Yapo kwa mbali ila sio yale seriously”

“Uta kuwa sawamke wangu”

Nikaaa ukweni hapa hadi majira saa mbili usiku kisha nikaondoka na kurudi nyumbani kwangu. Asubuhi na mapema nikawasiliana na Msuya na kumuomba tuweze kukutana ikulu pale inapo timu saa mbili asuhuhi na tukakubaliana katika hilo. Nikampigia mke wangu na kumjulia hali yake.

“Nimeamka poa mume wangu kipenzi”

“Sawa baby baadae nita kuja kukuona”

“Karibu mume wangu”

“Nashukuru”

Mara baada ya kumaliza kuzungumza na mke wangu, nikajianda na kuelekea ikulu. Nikawahi kumkuta Msuya akinisubiria eneo la karibu la ikulu. Nikaongozana naye hadi ndani ya ikulu. Tukaelekea nyumbani kwa raisi kwa ajili ya mazungumzo juu ya Msuya kuchukua nafasi yake. Tukasalimiana na raisi pamoja na mke wake kisha mazungumzo yakaanza.

“Niwaandalie kifungua kinywa?”

Mke wa raisi alituuliza kwa sauti ya unyenyekevu.

“Ndio madame”

Nilijibu mimi kwa maana nyumbani kwangu sija pata kifungua kinywa.

“Hembu igiza sauti yangu”

Raisi alimuambia Msuya na akaigiza sauti anyo izungumza raisi hadi yeye mwenyewe akashanga. Hata mke wake ika mbidi kutoka jikoni na kuja kumsikiliza Msuya jinsi anavyo zungumza.

“Kwa kweli Mungu amekupa karama ya kipekee sana”

Mke wa raisi alizungumza kwa furaha.

“Nashukuru mdame”

“Eddy kweli hapa ume fanya kazi. Jana usiku nilizungumza na wataalamu wa kutengeneza maumbo hayo ya bandia. Hivyo kesho wata kuwa na sample kumi na wata zileta hapa ikulu kwa siri sana”

“Sawa muheshimiwa. Ningependa nikuache wewe na Msuya hapa, kuna sehemu nina hitaji kueleke. Nina imani mukikaa siku nzima hii kuna mambo mengi sana ana weza kuyajua kwako, hususani watu wako wa karibu ambao una imani kwamba wata kuwepo nchini Ujerumani na wata taka kuzungumza na wewe”

“Ni kweli hata hilo jana mke wangu aliniuliza kwamba endapo ata kutana na marafiki zako na watapigisha stori si ita kuwa mtihani, nashukuru kwa kuwa nawe ume weza kulipatia uvumbuzi Eddy”

“Ni jukumu langu na nita hitaji kukuangalia walinzi ambao wata ambatana na wewe. Usishangae wakawa sio walinzi wako wa hapa ikulu”

“Sawa nina kusikiliza wewe tu kwani ndio ninaye kuamini”

“Nashukuru”

Nikaaga na kuondoka, nika anza safari ya kuelekea Bagamoyo kwenye nyumba yangu ya siri. Machale yakaanza kunicheza mara baada ya kuona gari nyeusi aina ya VW ikinifwatilia toka nilipo kuwa mataa ya Mwenge na sasa nina imalizia Tegeta.

‘Hawa Kenga kama hawanijui nita dili nao’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikipapasa kiunoni mwangu na kuikuta bastola yangu ikiwa ime tuna vizuri na nilisha iandaa tayari kwa kazi yoyote toka pale nilipo kuwa nimetoka nyumbani kwangu asubuhi.



Nikazidi kusonga mbele huku nikiwa makini sana. Nikapata wazo la haraka, nikatoa simu yangu mfukoni na kumpigia simu Willy.

“Dogo kuna namba za gari moja hivi lina nifwatilia, ziandike hapo alafu unitumie taarifa zake kwenye simu yangu”

“Sawa kaka”

Nikamtajia Willy namba za gari linalo nifwatilia kisha nikaendelea na safari yangu kana sijawastukia chochote wanao nifwatilia. Nikafika kwenye moja ya sheli, nikaigia na gari hilo likapita na kusimama kwa mbali kidogo.

‘Wajinga wana niwinda’

Willy akaitumia taarifa za gari hili linalo milikiwa na bwana Selemani Selemeani anaye ishi Dar es Saalam”

“Dogo”

Nilizungumza huku simu yangu ikiwa sikioni.

“Ndio kaka”

“Huyo mmiliki wa hilo gari ana jishuhulisha na nini?”

“Ni mfanya biashara tu wa kawaida”

Nikashuka kwenye gari na kuingia kwenye supermakert ndogo iliyopo sheli hapa.

“Okay nitakupa mrejesho”

“Kwani upo kwenye hatari?”

“Naona kuna mkia una jaribu kunifwata”

Nilizungumza huku nikimtazama muhudumu wa kike hu mkononi mwangu nikiwa nimeshika soda za kopo za Cocacola. Nikaziweka juu ya meza ya muuzaji huyu.

“Kuwa makini kaka”

“Usijali, kama kweli kile ninacho kiwaza ndio wanacho jaribu kukifanya basi hakuna hata mmoja atakaye rudisha ripoti kwa bosi wake”

“Kama uta hitaji msaada niwajulishe Maulid na Judy”

“No wala usiwasumbue”

“Sawa kaka”

Nikakata simu na kuiweka mfukoni.

“Hi mrembo habari yako”

“Salama kaka”

“Una itwa nani?”

“Mariam”

“Waoo una jina zuri kama wewe ulivyo mzuri”

“Hahaaa nashukuru”

Nikatoa noti nne za shilingi elfu kumi na kumkabidhi.

“Nyingie uta kunywa soda”

“Asante”

“Muna funga saa ngapi?”

“Saa kumi na mbili”

Nikatazama saa yangu ya mkononi, ina nionyesha ni saa tano na dakika kumi na mbili.

“Nita rudi, kwa ajili yako au ume olewa?”

Nilimtania Mariam ambaye kwa kweli ana sura nzuri.

“Hahaaa kawaida”

“Sema kama ume olewa nisije si una jua bwana shemeji ana weza kunipiga mangumi”

“Hahaaa hakuna bwana wewe kuwa huru”

“Sawa”

Nikambusu busu la hewa na kumfanya acheke. Nikarudi nilipo liacha gari langu.

“Nimejaza full tank mzee”

“So ume ongeza ngapi?”

“Lita ishirini”

Nikampa kijana huyu wa benk kisha nikaondoka zangu. Nikalipita gari hili linalo nifwatilia kwa mwendo wa taratibu na nikafanikiwa kuona idadi ya watu waliomo ndani ya gari hilo japo vioo vyake ni vyeusi. Mbele amekaa dereva na mwanaume mmoja huku nyuma wakikaa wanaume wawili. Nilipo fika mita hamsini nao wakaanza kunifwatilia.

“Haaa…..hawa majamaa mbona mandezi sana. Kunifwatilia gani huko hadi nina jua”

Nilizungumza kwa dharau kwa maana inavyo onyesha hawajui hata wanaye mfwatili ni mtu wa aina gani. Nikaanza kuongeza mwendo kasi wa gari langu huku nikizipita gari kadhaa ambazo zipo mbele yangu, nao waka fanya mchezo nilio ufanya mimi wa kuyapita magari hayo. Nikazidi kuongeza mwendo na nikafika eneo ambalo halina makazi ya raia na hakuna magari yanayo pita kwa sana. Nikapunguza mwedo na kuwafanya na wao kupunguza mwendo. Nikaichomoa bastola yangu ya kiunoni, nika iweka katika siti ya pembeni, nika simamisha gari langu galfa na kuwafanya wanipite. Nikachukua bastoka yangu na kushusha kioo cha upande wangu nikatoa mkono wangu wa kulia na kupiga risasi ipiga tairi ya nyuma ya upande wa kulia na kusababisha gari hilo kuanza kuyumba huku dereva akijitahidi kuhaikisha ana liweka sawa. Nikaliondoka kwa kasi gari langu na kuana kuwafwata, nikawakaribia kupiga risasi tairi jengine la kushoto na gari likapoteza muelekeo na kutoka nje ya barabara na kuanza kubingirika mara tatu na likatulia, matairi juu huku likifuka moshi mwingi. Nikashuka na kuwasogelea kwa umakini huku bastola yangu ikiwa mkononi. Mmoja wao aliye kaa siti ya nyuma akajitahidi kutoka ndani ya gari hili huku akiwa na bastola mkononi ila tayari nikamfikia na bastola hiyo nikaipiga teke ikaangukia pembeni.

“Nyinyi ni kina nani?”

Nilimuuliza kwa ukali sana. Akanitazama kwa macho ya jazba. Nikaichukua bastola yake nikawachungulia watatu walio salia ndani ya gari hilo na hali zao zipo hoi huku huyu aliye jitahdi kutoka nje naye damu zikiwa zina mwagika usoni mwake. Nikampapasa haraka haraka mfukoni mwake na kutoa wallet yake pamoja na kiasi cha pesa, nikampiga na kitako cha bastola yake usoni, kisha nikasogea mita kadhaa na kupiga risasi tanki la mafuta na kusabisha gari hilo kulipuka. Nikairushia bastola yake ndani ya gari hilo na wakaanza kuteketea kwa moto, nikasogea eneo la barabarani, hazikuisha hata dakika mbili gari mbili za abiria zikafika eneo hili na kusimama. Abiria wakashuka huku kila mmoja akiwa ana shangaa jinsi gari hilo linavyo teketea kwa moto. Baadhi ya abiria wakawapigia polisi simu na kuwataarifu juu ya ajali hiyo huku abiria wengine wakirekodi kuungua kwa gari hilo.

“Kaka ilikuwaje?”

Binti mmoja aliniuliza mara baada ya kuniona nipo kimya.

“Mwenyewe nilimelikuta lime pinduka na moto umesha samba gari zima hivyo nime shindwa hata kuwaokoa.”

Dada huyu akanitazama kwa macho ya udadisi hadi alipo fika kiunoni mwangu macho yakazidi kumtoka mara baada ya kuona bastola yangu nikiwa nime ichomeka eneo la mbele ya liuno changu.

“Mimi ni askari”

Nilizungumza ili kumtoa wasiwasi mwana dada huyu.

“Ahaa sawa”

Magari yakaanza kujaa eneo hili, nikaingia ndani ya gari langu na kuondoka, huku nikipishana na gari mbili za polisi pamoja na zima moto zikitokea Bagamoyo. Nikafungua wallet niliyo ichukua na kuanza kutoa kitambulisho komoja baada ya kingine. Kitambulisho cha kwanza ni cha urai wa nchini Kenya. Huku kadi mbili zikiwa ni za benki huku kadi moja ikiwa ni benk ya Tanzania na kadi ya pili ni beki iliyopo nchini Kenya.

“Mahaboud Abas Karani”

Nilisoma jina la mtu huyu. Nikafika katika nyumba yangu kisha moja moja kwa moja nikaelekea eneo la nyuma ya chini ilioyo ardhini. Nikapiga picha kitambulisho hichi na kumtumia Willy ili anitafutie taarifa kamili za huyu bwana Karani. Nikafungua moja ya chumba cha siri ambacho sikuwaonyesha Willy na wezake. Chumba hichi huwa tuma hifadhia nguo na silaha za kininja pekee. Nguo za wezangu watatu ambao wametangulia mbele za haki nazo zipo katika chumba hichi. Nikazitazama huku machozi yakinilenge lenga.

‘Hei ndugu zangu. Nina imani roho zetu hazija pumzika kwa amani. Nina waahidi nita dili na hawa Scorpion hadi nina wamaliza. Kama wao wana sumu, ila mimi peke yangu sumu yangu ita kuwa ni kali kuliko wao’

Nilizungumza maneno ya kujiapiza moyoni mwangu. Nikavua nguo nilizo vaa kisha nikazivaa nguo zangu ambazo zina mwaka wanne sasa hazijaugusa mwili wangu. Kitendo cha kumaliza kuvaa nguo hizi, damu mwili mzima ikanisisimka kwa maana nikahisi kama jini la kikatili ambalo lilikuwa limeniachia kwa miaka kadhaa sasa limesha rudi mwilini mwangu upya. Nikachukua silaha kadhaa ikiwemo upanga mrefu, imara na wenye kukata pande zote mbili na makali yake ni zaidi ya kiwembe kimya. Nikaingia kwenye moja ya chumba kikubwa cha mazoezi na nikaanza kufanya mazoezi ya kichina. Mazoezi ambayo ni makali sana, yanayo hitaji mtu kujitoa ufahamu wako na kujiona sio binadamu ila ni shetani. Nikajipima kasi ya kutumia upanga huu, nikajipima kasi ya kuruka hewani sarakasi ambazo una weza kwenda hata futi kumi na mbili, mazoezi haya huwa yana tusaidia sana katika kuruka kuta ndefu. Mazoezi ya lisaa moja yakanitosha, kisha nikafanya sala ya kininja ambayo ina hitaji utulivu na hisia kali sana. NIkamaliza kufanya sala hii ambayo huwa si ya kumuomba Mungu ila ni ya kuomba mizimu ya kijapani ya kabila la Samurai kuweza kunisaidia katika kazi zagu hizi. Mara baada ya kumaliza mazoezi haya nikavua nguo hizi na kuziridisha sehemu zake pamoja na silaha nikaziweka vizuri. Nikaingai bafuni na nikaoga kwa haraka kisha nikavaa nguo zangu nilizo kuja nazo eneo hili. Nikakuta missed call tatu za Willy na ikanibidi nimpigie.

“Dogo”

“Ndio kaka nime fanikiwa kuweza kupata taarifa za mtu huyu Kamara. Alikuwa ni special force wa jeshi la Kenya na aliweza kuachishwa jeshi kutokana na makosa ya utovu wa nizamu. Hivyo akajiunga kwenye kikundi kimoja kiitwacho THE ONE. Kikudi hicho kazi yake ni kufanya mauaji na hapo kuna mchanganyiko wa wanajeshi na majasusi mbalimbali”

“Ina maana walilipwa ili waniue?”

“Ndio kaka, ila vipi upo salama kwa maana lingepita lisaa moja na nusu ninge wataarifu Maulid na Judy wakufwatilie?”

“Nipo salama alafu jamaa nina hisi aliye watuma hakuwapa full details zangu ndio maana walikurupuka kwenye kunifwatilia?”

“Vipi kwani umewamaliza?”

“Duu muda mrefu hadi nimeshau kama nime ua. Kuna video nahisi zitakuwa zinasambaa mitandaoni za gari linalo teketea kwa moto na watu wake ndani”

“Ohoo nimeiona kumbe ndio wale, ime tokea njia ya kwenda Bagamoyo?”

“Yes ndio hao hao”

“Duuu pole sana kaka”

“Pole yao kwa maan hajawarejesha mrejesho kwa Boss wao. Una weza kujua nini aliye wapa kazi ya kuniua?”

“Mmmm hapo ni ngumu kaka kwa maana hawa jamaa wapo kwa siri sana”

“Poa, nitafutie mmiliki wa hilo gari”

“Ana patikana Kariakoo kuna duka la vifaa vya magari ana uza”

“Poa ngoja nika onane naye sasa hivi, nitumie picha yake”

“Hakuna shaka kaka”

Nikakata simu na kuondoka nyumbani hapa, nikiwa njiani Willy akaninitumia picha kadhaa za bwana Selemani Selemani. Majira ya saa nane kasoro nikafika katika super makert nilipo nunua soda za kopo.

“Nimerudi Mariam”

“Weee kumbe ulikuwa seriously?”

“Yaa au ulihisi nina kutani?”

“Yes”

“Ohoo basi pole yako”

“Nashukuru”

“Ehee una muda?”

“Nipo job na nina toka saa kumi na mbili na nusu jioni”

“Niachie basi namba yako ya simu”

“Mmmm naona una pete ya ndoa mkooni kweli mke wako hato kuchinja akiona namba yangu?”

“Hawezi, kwanza hana muda wa kushika simu yangu”

“Ila wanaume wa watu nyinyi nina waogopa”

“Usiniogope bwana. Wewe nipatie au nikupe yangu”

“No wewe chukua yangu”

“Kwani una ishi wapi?”

“Maeneo haya haya ya hapa Tegeta”

“Muda wa mwisho kukupigia simu ni saa ngapi?”

“Muda wowote kwa maana nina ishi na dada yangu”

Mariam akanitajia namba yake ya simu na nika ihifafadhi(save) kwenye simu yangu.

“Nashukuru, nita kupigia leo usiku, uniambie ni wapi nikufwate”

“Ila una itwa nani?”

“E”

“E”

“Ndio”

“Haina kirefu?”

“E.D.D.Y”

“Mmm ndio jina gani?”

“Eddy”

“Ahaa sawa, ni beep ili niwe nawe na namba yako”

“Sawa”

Nikafanya jinsi Mariam anavyo hitaji. Sikuzote wasichana kama hawa ni wepesi sana kuwapata kwani wengi wao wana tazama pesa na maisha mazuri ya mtu. Nikaagana naye na kuingia kwenye gari langu na kuendelea nasafari yangu huku Mariam nikimuweka kama kipozeo pale mambo yatakapo nivuruga. Nikafika Kariakoo na nikaingia katika duka la bwana Selemani Selemani na kwa bahati nzuri nika mkuta akiwa na wafanyakazi wake wanne huku wateja wakiwa wameshamiri.

“Karibu sana bosi”

Kijana mmoja alinikaribisha kwa furaha.

“Nashukuru, nina muhitaji bosi wako”

Akanionyesha bosi wake ambaye tayari nimesha mfahamu kupitia picha. Nikasalimiana naye kwa kupeana mikono.

“Nina weza kuzungumza nawe private?”

“Yes karibu sana ofisini kwangu”

Tukaingia ofisini kwake na nika kaa kwenye kiti cha wageni.

“Nina itwa bwana Eddy, kuna gari yako moja nyeusi ina ya VW”

“Yaa ni gari yangu hiyo”

“Ahaa ina fanyia kazi gani gari yako?”

“Ni moja kati ya magari ambayo nina yakodisha kwa watu private. Nina mradi huo wa kukodisha magari kwa watu ambao huja mjini hapa kwa shuhuli zao binafsi basi nina wakodishia kwa masaa, siku na kuendelea”

Bwana Selemani alizungumza na jinsi ninavyo msoma ana onekana kwamba hatambui watu alio wakodisha ni kina nani, nika mtajia namba za gari lake na kumuomba majina ya watu walio mkodisha.

“Ahaa kukupatia majina nita kupatia, ila tutambuane kwanza ndugu yangu kwa maana kutoa taarifa za wateja wangu kwa watu ambao siwafahamu kidogo ni shida”

“Mimi ni mpelelezi wa serikali”

“Naweza pata kitambulisho chako”

“Ndugu nime zungumza nawe kiwema kwa ajili ya kwamba nina hitaji kujua hao watu ulio wakodisha ni kina nani. Hivi hujiulizi nime kujuaje, hujiulizi kwa nini nipo hapa na nina pica zako na details zako kuanzia tarehe uliyo zaliwa hadi sasa. Hivyo tusifikishane mbali, nipe nilicho kuomba niondoke kwa wema”

Bwana Selemani macho yakamtoka ili kumdhibitishia kwamba nina mfahamu vizuri nika muonyesha picha zake, akavuta kitabu kilichopo pembeni yake na akakifungua kurasa kadhaa na kuionyesha jina la mtu aliye kodisha gari hilo.

“Halima Salum?”

“Ndio, ni dada mmoja kutokea Kenya”

“Namba anayo itumia ndio hii?”

“Ndio”

“Kwa sasa nina weza kumpatia wapi?”

“Nina weza kukupa ushirikiano wa kumpigia kwa maana sitaki matatizo ndugu yangu. Mimi ni mtu mwema na nina ogopa sana polisi”

“Sawa fanya hivyo”

Akatoa simu yake kwenye mfuko wake wa kanzu na kumpigia mwana dada huyo. Simu ikaanza kuita kwa muda kisha ikapokelewa.

“Halima upo wapi ndugu yangu?”

“Nipo hotelini nime jipumzisha, vipi mbona una uliza au una taka kunibadilishia gari?”

“Hapana kwa maana hiyo gari haina shida?”

“Sele ndugu yangu jana si nilikuambia kwamba nina taka ile BMW X5, ukasema ita letwa leo”

“Ndio, ila ikija nita kujuza ndugu yangu”

“Sawa nashukuru”

Bwana Selemani akakata simu huku nikiwa nime yasikia mazungumzo yao kwani aliweka loud speaker katika simu yake. Bwana Selemani kama alivyo sema hataki shida na polisi na ana waogopa, akaniandikia jina la hoteli na chumba alichopo Halima Salum, nikaagana naye na kuondoka eneo hili na kwa bahati nzuri Hoteli yenyewe ipo hapa hapa Kariakoo. Nikafika hotelini na nikaingia katika lifti iliyo nipeleka hadi gorofa ya tano, nikatembea kwenye kordo hadi chumba namba elfu moja na moja. Nikaminya kengele ya chumbani hichi na baada ya sekunde kadhaa mlango ukafunguliwa na mbele yangu akasimama mwana dada mrefu, mweupe na mwenye umbo namba nane huku mwili wake huu nilio utathimini haraka haraka, akiwa ameuziba kwa kijitaulo kidogo tu ambacho kimeyafanya mapaja yake meupe na yaliyo nona kuonekana vizuri tu machoni mwake hadi nikajikuta nikiyatamani nikiwa kama mwanaume lijari niliye kamilika kila idara.



“Habari yako”

Halima Salum aliniuliza kwa sauti nyororo huku akinitazama usoni mwangu kwa macho yaliyo jaa udadisi mwingi sana.

“Nina imani kwamba wewe ndio Halima?”

Halima akaka kimya huku akitafakari kujibu swali hilo.

“Nina maswali na wewe kadhaa, ninge penda kukuhoji kama huto jali”

“Kaka samahani sikufahamu”

“Okay nina itwa Eddy ni afisa upelelezi”

“Nime fanya kosa lolote?”

“Hapana huna kosa, ila kama hauto jali nina kuomba unikaribishe ndani”

“Kitambulisho chako?”

Nikatoa barua yenye muhuri wa raisi, akaisoma kidogo kishaa kanitazama usoni mwangu.

“Nita kuamini vipi ikiwa barua ina maelezo tu na haina pivha yako?”

“Dada nime zungumza nawe kiustarabu kwa maana nna hitaji kufahamu mambo kadhaa. Hivyo tuzungumze”

Nilizungumza kwa ukali kidogo huku huku nikichukua barua yangu anayo nirudishia Halima. Akaufungua mlango na nika ingia ndani huku yeye akifwata kwa nyuma. Nikatazama chumba hicho kwa sekunde kadhaa, kisha Halima, akakaa kitandani na kutafanya mapaja yake yazidi kuonekana vizuri.

“Una mfahamu Mahaboud Abas Karani?”

“Amefanya nini?”

“Sister sijaja kukubembeleza na hadi nime kuja hapa hotelini ina maana nime kufwatilia na nina kujua vizuri. So twende kiustarabu au nikubebe ukajibie maswali yangu kituoni na kumbuka wewe sio Mtanzania ni Mkenya”

“Sawa sawa kaka. Mahaboud ni mpenzi wangu”

“Muna muda gani kwenye mapenzi yenu?”

“Three month now”

“Ana jishuhulisha na nini?”

“Yeye ni mfanya biashara”

“Una jua ni wapi alipo?”

“Alitoka asubuhi na gari niliyo kodi na amekwenda ubalozi wa Kenya”

Nikatoa simu yangu mfukoni na kumuonyesha Halima detail za Mahaboud pamoja na picha zake akiwa katika jeshi la Kenya.

“Mwanajeshi?”

“Kwani hakuwahi kukuambia?”

“Hapana”

“Mume wako ni muuaji”

“Muuaji?”

“Ndio”

“A….memuua nani?”

Halima alizungumza kwa wasiwasi huku kijasho kembamba kikimwagika usoni mwake.

“Kuna watu alikuwa nao na walijaribu kumuua mmoja wa watu wetu. Ila kwa bahati mbaya aliweza kuzidiwa na wakauwawa. Hivyo nina hitaji uweze kuvaa nguo zako sasa hivi. Ili ukaweze kuitambua miili yao”

“Ohoo Mungu wangu. Weee kaka acha utani, Mahaboud wangu amefariki?”

“Sina utani na wewe. Vaa nguo tutoke”

Halima akanikodolea macho huku akiwa kama mtu ambaye haamini anacho kisikia. Nikasimama na kufungua kabati la nguo lililopo katika chumba hichi. Nikaona tisheti nyeupe pamoja na jinzi nyeusi ambazo ni nguo Halima. Nikamrushia Halima na kumpa ishara ya kuingia bafuni ili abadilishe nguo hizo. Taratibu akanyanyuka na kuingia bafuni huku akionekana hana hata nguvu ya kutembea. Baada ya dakika kama sita hizi Halima akatoka akiwa amevaa, akachukua vikandambili vya kisasa.

“Una chochote cha kubeba”

“Pochi yangu na simu”

Akababe pochi yake na tukatoka ndani hapa. Tukaingia katika gari langu kabla ya kuondoka nikampigia simu Willy.

“Dogo miili ya wale majambazi ime wekwa wapi?”

“Lugalo”

“Poa”

Nikawasha gari na kuondoka eneo hili. Ukimya ukatawwala ndani ya gari huku nikiwa nina waza watu ambao wapo nyuma ya tukio hili kwa maana nisipo kuwa makini nina weza kujikuta nina ingia kwenye mdomo wa mamba na nikashindwa kujitoa. Nikamtazama Halima na kumuona anamwagikwa na machozi ya kimya kimya huku naye akiwa ametawaliwa na mawazo. Nikatoa kitambaa mfukoni mwangu na kumkabidhi.

“Asante”

Halima alizungumza kwa sauti ya upole na iliyo jaa majonzi. Tukafika hospitali ya Lugalo, nikajitambulisha kwa daktari mkuu.

“Miili hiyo ni kweli ime fikishwa hapa na ipo Mochwari kwa sasa”

“Nina weza kuiona?”

“Ndio una weza kuiona ila ime haribika sana kwa moto”

“Hakuna shaka”

“Na yule dada ana ujasiri wa kuiona?”

Dokta alizungumza kwa sauti ya chini huku tukimtazama Halima ambaye ana onekana kimwili yupo hapa ila kimawazo na fikra hatupo naye kabisa.

“Sidhani, ila acha nikaione kwanza peke yangu”

Nikamuomba Halima aweze kunisubira eneo hili la kupumzikia ila akagoma na kutaka kujumuika nami.

“Sawa”

Tukaongozana na daktari mkuu hadi Mochwari. Tukakuta miiili ya watu wanne ikiwa imelazwa chini katika sakafu huku imefunikwa mashuka.

“Miili yao ni hii hapa”

Daktari alizungumza huku akitoa gloves nyeupa mikononi mwake na kuzivaa. Akafungua maiti ya kwanza, Halima akastuka sana na kunikumbatia glafa ili asiweze kuitazama. Dokta akutazama kisha nikampa ishara ya kuifunua miili mingine na akaendelea kufuna mwili mmoja baada ya mwingine na mwili ni wa Karani na yeye kidogo uso wake haujaungua sana kwa maana yeye alikuwa ametoka ndani ya gari kwa ajili ya kunidhuru mimi ila niliwahi kumdhibiti.

“Mpenzi wako si ndio huyu?”

Nilimuuliza Halima, taratibu akaugeuza uso wake na kuutazama mwili wa Mahaboud Abas Karani, akaanza kuangua kilio cha nguvu hadi ikanibidi nimtoe ndani hapa. Hatukufika hata nje, akazimia. Manesi na madaktari wakampakiza katika kitanda cha magurudumu na kumkimbiza kwenye chumba cha matibabu.

“Dokta nina hitaji mgongwa huyo aweze kuwekewa uangalizi sana kwani nina hitaji kupata baadhi ya mambo kutoka kwake”

“Sawa nime kuelewa”

Nikachukua pochi ya Halima, nikatoa simu yake aina ya Samsung S10+. Nikashindwa kuifungua kwa maana ina hitaji ufunguzi wa macho yake ndio ifanye kazi. Nikatoa simu yangu mfukoni na kumpigia mke wangu.

“Hei baby”

“Yes honey”

“Una endeleaje?”

“Nipo vizuri mwenzio nimesha anza kurembwa rembwa yaani wee acha tu. Vipi umesha kula?”

“Bado mke wangu, nita kuja huko kesho asubuhi”

“Sawa mume wangu, ila vipi kazi?”

“Nina mshukuru Mungu”

“Upo wapi sasa?”

“Lugalo”

“Kuna mgonjwa?”

“No kuna dokta nime kuja kuzugumza nae”

“Ahaaa, ila upo salama”

“Nipp salama mke wangu kama chuma”

“Nafurahi kusikia hivyo mume wangu. Sasa kabla ya kulala nita kupigia”

“Sawa baby”

“I love you”

“I love you too”

Nikakata simu na muda wa sasa ni saa mbili kasoro usiku. Daktari akanifwata na kunieleza kwamba Halima ametundikiwa dripu ya maji na baada ya masaa mawili ata zinduka.

“Okay saaa nne usiku nita kuwa hapa dokta”

“Hakuna shaka”

“Hii ni pochi yake na simu yake. Nita vikuta kwako”

“Sawa sawa”

Nikaondoka hapa huku kichwani nikiwa na mambo mengi. Nikiwa njiani simu yangu ikaanza kuita, nikaitazama na kukuta ni Msuya.

“John niambie”

“Poa kaka ndio nina toka ikulu sasa hivi. Aisee nime toka na madini ya kutosha kutoka kwa yule mzee nina uhakika hiyo siku watanikoma”

“Haahaa kwa hiyo ume weza kujua step zake na mambo mengine”

“Ndio kaka yaani kazi ime kwenda vizuri sana, yaani ina wezekana hata mimi ndio nikasimama kwenye huo mkutano si ana hotuba?”

“La hotuba silifahamu, ila ata kuwepo kwenye mkutano”

“Basi nita simama mimi nay ale maumbo ya bandia yanayo endana naye yamesha letwa”

“Safi kaka, nina kutegemea kwenye hii kazi”

“Usijali ndugu yangu, ngoja nikajifue zaidi ili kusiwe na utofauti wowote katika hili, alafu kuna hishu ya macho kidogo mimi mboni zangu sio nyeusi kivile ni kahawia, ina kuwaje hapo kaka?”

“Usijali kuna mboni za bandia na mboni hizi zita fanania na mboni zake na hata itakapo fika kwenye mambo kadhaa ya kufungua vitu ikiwa ina hitajika mboni yake basi tuta fanya hivyo”

“Sawa kaka. Ila nina shukuru sana kwa nafasi hii uliyo nipatia ndugu yangu nina imani sinto rudi tena kambini kule”

“Usijali kukubwa ni kusaidiana ndugu yangu”

“Sawa kaka usiku mwema”

“Nawe pia”

Nikakata simu, nikafika Mbezi moja na kuingiakweye moja ya mgahawa, nikaagiza chakula, huku nikiendelea kutafakari mambo mengi ya nchi hii.

‘Makamuwa raisi ndio kirusi kwenye hii nchi. Nikimuua sasa hivi sinto weza kuwajua kwa mapana hawa watu na akifa yeye ata patikana mrithi mwengine ambaye ana weza kuwa ndio kirusi zaidi ya makamu wa raisi’

Niliwaza huku nikitazama baadhi ya watu walipo katika mgahawa huu. Eneo nililo kaa mimi lina kigiza kidogo na sio rahisi kwa mtu kuweza kuniona.

‘Ila ina bidi niwafyeke mmoja baada ya mwengine tena si kwa kuwapiga risasi, lazima wafe kwa ajali.’

‘Ila wengine wapo nje ya nchi nita wezaje pasipo msaada?’

Hadi muhudumu ana weka chakula juu ya meza wala sikuwa hapa kimawazo.

“Kaka karibu”

Sauti ya msichana huyu ikanistua kidogo.

“Ohoo asante sana”

Akaondoka muhudumu huyu na nikaanza kula taratibu.

‘Baba mkwe ni miongoni mwao. Amesema yupo kwenye hatari. Mmmmm ni hatari gani au wamesha mfahamu kwamba ni msaliti?’

‘Ila kuwa karibu nami ndio kuna muweka hatarini’

‘Kama nime ingia kwenye hii kazi maisha ya Cauther yapo hatarini sana. Ila siwezi kumuacha kw amaana ni mke wnagu halali wa ndoa’

Nikiwa katika mawazo haya ya ndoa, nikamkumbuka Mariam niliye onana naye asubuhi. Nikajishauri kwa sekunde kadhaa kisha nikampigia simu.

“Ni mimi Eddy”

“Ohoo Eddy mambo?”

“Safi upo wapi?”

“Nipo nyumbani nimesha toka kazini?”

“Una weza kufika hapa Mbezi beach?”

“Muda huu?”

“Ndio kodisha hata bodaboda, uta mpatia simu na kumueleza akulete wapi?”

“Mmmm ila nina ogopa?”

“Una ogopa nini?”

“Sikujui, alafu una niita usiku huu, si una jua mimi mtoto wa kike”

“Acha hizo, muda bado kwa daa saa tatu kasoro hii una ogopa. Hembu njoo bwana, tupate chakula cha usiku”

“Sawa, ngoja nimuage sister, ila si sinto kaa sana?”

“Ndio”

“Sawa nita kupigia nikiwa nimesha mpata bodaboda”

“Poa, hembu kata simu kuna simu ina ingia kwangu”

Mariam akakata simu na nikaipokea simu ya Maria.

“Eddy mambo”

“Poa niambie”

“Safi, simu yako ipo busy sana?”

“Kuna mtu nilikuwa nina zungumza naye”

“Basi ngoja nikuache”

“Tuongee tu”

“Upo wapi?”

“Sehemue sehemu vipi?”

“Yaani Eddy nisiwe muongo wala mnafki nina hamu sana na wewe, yaani toka unionjeshe ile siku nimejikuta nina shindwa kabisa kukutoa moyoni mwangu. Eddy na…..”

“Maria ndio maana ile siku nilikataa kufanya na wewe kwa maana nilijua haya yote yata tokea. Hembu ukinipigia muda kama huu uwe na mambo ya kuzungumza hususani ya kazini ila sio ya mapenzi. Nina mke kwa mfano ana sikia unacho niambia ata fanya nini. Heshimu basi hilo”

Nilizungumza kwa msisitizo kidogo na kumfanya Maria kukaa kimya.

“Nita kupigia”

Mara baada ya kuzungumza hivyo nikakata simu kwa maana nikiendelea kuweka mazoea na Maria basi ndo yangu ita ingia matatani. Baada ya dakika kumi hivi, Mariam akanipigia simu na nikamuelekeza nilipo na kwa bahati nzuri akasema ana pafahamu. Baada ya dakika ishirini akafika, nikamuelekeza meza niliyo kaa, nikampatia pesa ya kumlipa muendesha pikipiki kisha akarudi. Kusema kweli huyu mtoto wa kike ame umbika, ana kila sifa ya kuitwa mwanamke mzuri.

“Ehee ulikuwa una hisi nita kuteke nini?”

“Mmmm hapana, ila si una jua nyinyi waume za watu bwana ni watu wa kuogopwa”

“Hahahaa usijali, una kula nini?”

“Chohote”

Muhudumu akafika hapa na Mariam akaagizia chakula anacho kihitaji.

“Una mri gani?”

“Mika ishirini na tano”

“Waoo bado mdogo sana”

“Yaa bado nina pambana na maisha ya Dar”

“Kwenu ni wapi?”

“Asili yangu mimi ni Mkaguru”

“Watu wa Morogoro”

“Yaaa”

Muhudumu akamletea Mariam chakula chake na tukaendelea kula huku tukipiga stori za hapa na pale. Ndani ya muda mfupi sana tukajikuta tume zoeana na Mariam kiasi cha kumtesti kumnyonya denda na akanikubalia.

‘Mtoto amesha lainika huyu’

Nilizungumza kimoyo moyo huku tukiachanishamidomo yetu na hichi kigiza cha eneo hili hakuna anaye weza kuona chochote. Nikatazama saa yangu ya mkononi na ina nionyesha ni saa nne kasoro usiku na muda huu wa saa nne ndio nilimueleza daktari kwamba nita fika hospitalini na mbaya sikuweza kuchukua namba ya dokta.

“Vipi tuna weza kulala usiku huu?”

Nilimuuliza Mariam na akatazama chini kwa aibu huku macho yakiwa yame mlegea, ikiwa ni ishara ya kwambaa na hitaji kutulizwa mzuka wa mapenzi ambao tayari umesha mpanda na endapo nikimuacha hivi hivi ana weza kunichukulia ni mwanaume suruali.



“Mke wako yupo wapi?”

“Ehee?”

Nilijibu huku nikiendelea kumtathimini Mariam kuanzia usoni mwake hadi kifuani mwake. Chuchu zilizo nona zikazidi kunipagawisha na kunifanya shetani wa nguno na wa kumsaliti mke wangu azidi kunitawala.

“Nimekuuliza mke wako yupo wapi hadi sasa hivi upon je na una kula mgahawani?”

“Ohoo amesafiri”

“Kaenda wapi?”

“Mbona una maswali mengi?”

“Nina uliza kwa maana hapa mjini bwana. Kuwa na mume wa mtu ina garimu. Mwaka juzi kuna rafiki yangu alimwagiwa tindikali usoni kwa sababu ya kutoka na mume wa mtu”

“Usijali mke wangu hawezi kufanya huo ujinga na pia hawezi kutambua hilo. Au uta simama na kuitangazia duania kwamba nina tembea na mume wa mtu?”

“Mmm nitaanzia wapi Eddy”

“Sasa sikia, nitakupitisha katika moja ya hoteli kisha nitakuacha, nina kwenda hospitalini kumtazama mgonjwa na baada ya hapo nita rudi hoteli”

“Mmmm hapana kwa kweli?”

“Nini sasa?”

“Usije ukawa una kwenda kuchukua wezako mukanipiga mtundo?”

“Mariam unanichukuliaje mimi? Au una nihisi kwamba mimi ndio wale vijana wa vijiweni wahuni wahuni au?”

“Hapana Eddy kama nime kuudhi nisamehe ila kwa maisha ya sasa hivi simuamini mtu hususani mwanaume”

Nikatoa wallet mfukoni na kutoa laki moja na nusu na kumkabidhi Mariam.

“Siku ambayo uta niamini uta nitafuta. Usiku mwema”

Nikanyanyuka huku nikimuacha Mariam akinishangaa. Nikapitia kaunta, nikalipa chakula na vinywaji tulivyo tumia na nikaondoka mgahawani hapa kwa maana niki muendekeza huyu Mariam kuna mambo muhimu hayato kwenda. Nikafika hospitali ya Lugalo na moja kwa moja nikaelekea katika wodi aliyo lazwa Halisa Salimu na nikamkuta nesi akibadilisha dripu la maji.

“Habari yako?”

“Salama kaka”

“Hali ya mgonjwa wangu ime fikia wapi?”

“Alizinduka majira ya saa tatu, akazimia tena ila tuna imani hadi asubuhi ana weza kuwa vizuri”

“Hiyo ni dripu ya ngapi?”

“Ya nne”

“Sawa”

Nikavuta kiti kimoja kilichopo ndani hapa na nikaaa.

“Daktari mkuu yupo?”

“Yupo kwenye chumba cha upasuaji sasa hivi

“Ana weza kutoka saa ngapi?”

“Sifahamu kwa kweli kwa maana ameingia kama dakika ishirini zilizo pita”

“Sawa”

“Wewe ni nani kwa mgonjwa?”

“Mume wake”

“Ohoo sawa”

Ilinibidi kumdanganya nesi huyu ili kuepukana na maswali mengi. Nesi akamaliza kazi yake na akatoka ndani hapa na akaniacha na Halima. Nikatoa simu yangu mfukoni na kuisoma meseji kutoka kwa Mariam akiniomba msamaha. Nikaachana na meseji hiyo na nikampigia simu Cauther.

“Vipi mke wangu ume lala?”

“Hapana mume wangu, nina zungumza zungumza na kina bibi hapa”

“Ahaa”

“Wewe upo wapi?”

“Bado nipo Lugalo”

“Mmmm ni nani huyo anaye umwa?”

“Kuna mtu mgonjwa nahitaji kupata information kutoka kwake. Si una jua mambo ya kazi”

“Ohoo nime elewa mume wangu”

“Yaa ndio maana nipo naye cse kuna watu wana muwinda, wana weza kummaliza kabla ya kupata taarifa hizo hapa alipo amezimia”

“Ahaa sawa mume wangu. Pola kwa kazi”

“Nashukuru sana mke wangu. Vipi maandalizi yamesha malizika?”

“Yaa yame malizika hapa tuna subiria kesho kutwa tufunge ndoa mume wangu”

“Mungu atubariki”

“Amen”

“Sawa mume wangu baadae ukitoka huko naomba unipigie”

“Poa.”

Nikakata simu mara baada ya kumuona Halima amefumbua macho yake. Nikasimma na kumsogelea.

“Hei vipi?”

“Nipo wapi hapa?”

“Upo hospitalini. Una nikumbuka?”

“Ehee”

“Unajisikiaje?”

“Ime kuwaje kwa mpenzi wangu?”

Halima alizungumza huku machozi yakimchuruzika mashavuni mwake. Nikakosa jibu la kumpa, taratibu nikamsaidia na akaka kitako huku nikimuwekea mto mgongoni mwake ili aweze kuegemea vizuri kitandani. Nafasi ya kitanda iliyo salia, nikaka huku nikimtazama.

“Halima”

“Beee”

Kabla sijamjibu chochote daktari mkuu akaingia ndani hapa huku akiwa ameshika pochi ya Halima.

“Amezinduka?”

“Yaaa”

Akanikabidhi pochi hiyo huku akinitazama.

“Una jisikiaje dada?”

“Nafuu”

“Tuna weza kuzungumza ndugu yangu”

Daktari aliniambia, nikanyanyuka na kuiweka pochi hii mezani na tukatoka ndani hapa na daktari.

“Ndugu yangu kwa sasa nina kuomba sana uweze kujaribu kumuweka mgonjwa kwenye mazingira ya kuto kumkumbuka maiti aliye muona hadi akapelekea kufariki duniani. Na kuna askari wapelelezi wamefika hapa walikuwa wana hitaji kuzungumza na huyo msichana”

“Wametoka wapi hao askari?”

“Makao makuu”

“Wamefahamu vipi kwamba msichana huyu yupo hapa?”

Nilimuuliza daktari huku nikimkazia macho.

“Walikuja kunihoji kama kuna ndugu walio jitokeza kuitazama miili ya zie maiti walizo zileta hivyo nikawalezea juu yako na juu ya huyu msichana”

“Wame kuja muda gani?”

“Kama dakika kumi hivi, kwa maana walikuwa wakinisubiria nitoke katika chumba cha upasuaji. Ili wanihoji”

“Waite nita wasubiria hapa mlangoni”

“Sawa”

Daktari kuu akaondoka na nikarudi katika chumba hichi na kumtazama Halima usoni mwake jinsi alivyo jawa na masikitiko na mkononi mwake amaeshika simu yake.

“Sikia kuna askari wana kuja nina hitaji chochote watakacho kuuliza usijibu. Umenielewa?”

“Ehee?”

“Tumeelewana?”

“Ndio”

“Poa”

Nikatoka ndani hapa, huku nikiwa makini sana kwa maana hadi sasa hivi sijajua maadui zangu wana mtandao gani. Nikaona wanaume wanne walio valia nguo za kiraia wakiwa wameongozana na daktari mkuu. Wakafika katika sehemu nilipo simama.

“Ndugu ni hawa hapa”

“Habari yako kijana?”

Mzee mmoja wa kamako alinisalimia huku akinipa mkono, nikatazama kiganja chake kwa ksekunde kadhaa na mkono wake wa pili wa kushoto ameshika simu ya upepo(redio call).

“Salama tu. Shikamoo”

“Marahaba”

“Sisi ni maaskari kutoka kitua cha kati. Tuna mazungumzo kidogo na wewe pamoja na mwanamke ambaye tume ambiwa na daktari”

“Naombeni vitambulisho vyenu”

“Aisee mbona una kiburi hivyo. Tume kuongelesha kiwema alafu una zungumza kwa kiburi?”

Askari mwengine aliye simama upande wangu wa kushoto alizungumza huku akinitazama machoni mwangu.

“Nami nime ongea kistarabu au nime wafokea. Na pia ni haki yangu kuona vitambulisho vyenu kwa maana siwezi kuhojiwa chochote na mtu nisiye mjua.”

“Chacha, acha hizo”

Mzee huyu alimzuia kijana wake aliye hitaji kunishika mkono, akatoa kitambulisho chake na kukikabidhi mkononi na kweli ni kitambulisho cha askari wa jeshi la polisi Tanzania. Nikasoma maelezo yake kisha nika mrudishia.

“Na nyinyi nina omba vitambulisho vyenu”

“Kijana hatuna muda wa kupoteza”

“Mzee nimeona chako, hawa watatu nao wanipe”

Wakatazamana huku wakionekana kuchukizwa na ujasiri wangu, kwani wamesha zoea wananchi wa kawaida wakisha ambiwa kwamba sisi ni askari basi wana tetemeka kiasi cha kushindwa kujua haki zao wanazo paswa kudai kwa askari hao.

“Nipatieni la sivyo hamto weza kuingia ndani hapa”

“Sawa”

Wakatoa vitambulisho vyao kishingo upande..

“Nashukuru kuwajua”

Nilizungumza huku nikimtazama kiongozi wao ambaye ni Inspecta Kabelwa.

“Tuna hitaji kuwahoji wewe na huyo mwanamke”

“Mimi ina tosha”

“Kwa nini wewe peke yako?”

“Hali ya mgonjwa sio nzuri”

“Ni kweli, mgonjwa ana zimia kwa mara kadhaa hivyo mungempatia muda labda hadi kesho asubuhi tuna himani kwamba hali yake ita kuwa salama”

Dokta alijazilishia kwenye jambo hilo na kuwafanya askari hawa kukubaliana naye.

“Una itwa nani?”

“Eddy”

“U mkazi wa wapi?”

“Hapa hapa Dar”

“Dar kwani hakuna maeneo?”

Askri mwengine alizungumza kwa ukali kidogo, nikamtazama kisha nikaachia msunyo mdogo.

“Oya ume nisunya?”

Askari huyu ambaye mwenye cheo cha Koplo alizungumza huku akijaribu kunishika bega.

“Mkuu waambie vijana wako wawe na heshima”

“Tuliani”

Mkuu wao alimtuliza kijana huyo kisha akaendelea kunihoji.

“Marehemu tuliweza kuwakuta na bastola sita pamoja na risasi zipatazo mia na ishirini. Je una mahusiano nao vipi marehemu?”

“Sina mahusiano nao kwa maana na mimi nina hitaji kufahamu ni nani aliye watuma kuniua”

Askari wote na daktari wakajawana mshangao.

“Walihitaji kukuua?”

“Ndio”

“Kwa nini wahitaji kukuua?”

“Inspectar. Labda niwaambie jambo moja ambalo halifahamu ili tusipotezeane muda. Mimi ni L.J wa jeshi, so nipo kazini na mimi na ninge penda muweze kukaa mbali na hii kesi kwa maana mimi ndio niliye jibu mashambulizi hadi wao wakapinduka na gari hilo mara baada ya kunishambulia. Huyu mwanmke niliye naye nina hitaji kufahamu ni nani na nani ambaye mume wake aliweza kuchukua kazi kwao kwa ajili ya kuniua”

Askari wakatazamana na wote wakanipigia saluti ya kubana mikono kwa maana nina cheo kupita wao na siku zote cheo changu huwa sipendi kukiweka wazi kwa watu.

“Sawa mkuu, tuna kuomba pale utakapo wapata wahusika uweze kuwasiliana nami, hii ndio namba yangu ya simu”

Inspectar akanikabidhi kadi yenye namba yake ya simu.

“Nashukuru”

“Ila ndugu yangu cheo hicho ume kipata ila ina onekana umri wako ni mdogo kuliko cheo chako?”

“Aliye kuambia jeshini umri ndio cheo ni nani, au kwenu huko ndio muna pewa vyeo kutokana na umri?”

“Hapana mkuu”

“Sasa. Hivyo nina shukuru kwa muda wenu, alafu kijana uache dharua kwa watu musio wajua, ipo siku muta mkuta mtu kwenye bad mood kisha muta tafuta matatizo yasiyo ya kilazima”

“Samahani kwa hilo mkuu”

“Asanteni kwa muda wenu”

Askari hawa wakaondoka huku walicho kuwa wamekifwata wamekikosa. Nikaingia ndani ya chumba hichi na kumkuta Halima akiwa amekaa kitandania.

“Nahitaji kurudi hotelini muda huu”

“Ila hali yako sio nzuri”

“Najisikia vizuri, nina hitaji kurudi hoteli. Tafadhali nirudishe”

Halima alizungumza huku akichomoa sindano ya dripu. Akashuka kitandani na kuvaa vikandambili vyake, akabeba pochi yake na kusimama wima kunidhihirishia kwamba yupo salama.

“Poa”

Tukatoka chumbani hapa na nikalipa pesa ya matibabu na kuondoka eneo hili.

“Ina maana Karama alikuwa ni jambazi alafu ana jiweka karibu na mimi?”

Halima alizungumza ikanibidi kumtazama.

“Ndio”

“Sasa nina anza kupata picha”

“Picha gani?”

“Una jua mapenzi yangu mimi na yeye yalianza galfa sana na nilijikuta nikimuelewa kwa kila jambo. Sasa marafiki zake ambao alikuwa ana niambia ni wafanya biashara wezake walikuwa wana nipa wasiwasi na juzi aliniambia kwamba nimkodishie gari kwa jina langu kwa maana na mizunguko ya hapa jijini. Kutokana ni mpenzi wangu niliamua kumkubalia tu”

“Umekutana naye wapi?”

“Kwenye baa moja jijini Nairobi”

“Katika kipindi hicho cha miezi ya mapenzi yenu. Je ulisha wahi kumuna na silaha?”

“Yaa ni jambo la kawaida kwa mfanya biashara yoyote kwa maana hata mimi nina bastola yangu kwa ajili ya ulinzi wangu binafasi”

Tukafika hotelini na moja kwa moja tukaelekea katika chumba chake.

“Begi lake la nguo nina weza kuliona?”

“Ndio, ngoja nikutolee”

Halima alizungumza huku akifungua kabati na akatoa begi dogo la nguo. Nikalifungua na kukuta hati ya kusafiria, nikaifungua na kuisoma kidogo. Nikazimwaga nguo zote kitandani na kuanza kuichambua nguo moja baada ya nyingine.

“Una tafuta nini?”

“Simu au laini ya siri ambayo huwa ana itumia pasipo mtu mwengine kufahamu”

Nikafungua vifuko vya nje ya begi hili na sijaona chochote, nikafungua vifuko vya ndani vya hili begi pia sikuweza kuona chochote. Katika kupitisha pitisha kiganja changu ndani ya begi hili nikagusa kitu kidumu kidogo ambacho moja kwa moja nika fahamu ni simu, ambayo ime ingizwa katika kitambaa cha ndani ya chegi hili na sio rahisi kwa mtu kuiona hata pale atakapo mwaga nguo zake. Nichana kitambaa hicho na kutoa simu hii ndogo aina ya Nokia ali maarufu, Nokia Obama. Nikaifungua mfuniko wa nyuma na kuikagua betri yake kwa maana simu hizi mara nyingi huwa zina uwezo wa kutumika kama bomu na pale tu unapo iwasha pasipo taadhari ina lipuka. Nikaifunga vizuri simu hii huku muda wote Halima akinitazama ninacho kifanya. Nikaiwasha na nikasubiria ianze kuwaka. Nikaanza kuipekua na namba ya mwisho iliyo piga katika simu hii, imepigwa siku mbili nyuma na inatokea nchini hapa hapa Tanzania. Nikampigia simu Willy na kumtajia namba ya simu hiyo ili aweze kunifafanulia ni namba ya nani. Baada ya dakika kumi Willy alanipigia simu.

“Kaka nime jaribu kui trace hii namba ila kwa bahati mbaya haionyeshi ni ya nani na haijasajiliwa, nime jaribu kuingia kwenye mfumo wa mtandao wa namba hii ili kuweza kufahamu ni simu ngapi zilizo pigwa, ila sijafanikiwa kabisa kuweza kujua ina husika na nani?”

“Haionyeshi hata mara ya mwisho iliwekwa kwenye simu ya nani?”

“Hapana haionyeshi”

“Hembu niione”

Halima alizungumza huku akiichukua simu niliyo ishika na kuitazama namba hiyo.

“Dogo baadae”

“Poa kaka”

Halima akaitazama kwa sekunde kadhaa kisha akaonekana kama ana vuta kumbukumbu.

“Hii siku nilimkuta akizungumza kwa siri chuoni, nilipo muuliza akaniambia kwamba ana zungumza na maamu wa raisi kuna kazi amempatia hivyo sija jua kama ni makamu wa raisi wa Kenya au wapi kwa maana nakumbuka ilikuwa ni saa sita mchane ndio nilimkuta akizungumza na simu hii ndogo na kuanzi majuzi sikumuona nayo na sikutaka kumfwatilia na mambo yake”

Nikashusha pumzi nyingi, huku sasa nikiwa nimesha pata mwangaza wa jambo hili kwamba aliyopo nyuma ya hili jambo ni makamu wa raisi ambaye tayari nimesha mpa onyo ambalo nahisi sasa analipuuzia.



“Okay nashukuru, upo Tanzania hadi lini?”

“Siwezi kuendelea kukaa Tanzania itanibidi nikalipe gari la watu kisha niondoke zangu hata kesho mchana.”

Nikatazama saa yangu ya mkononi na ina onyesha sasa ni saa nane usiku.

“Sawa ina bidi niondoke”

“Samahani kaka Eddy nina ogopa kuendelea kukaa hapa peke yangu. Nina kuomba sana kama hauto jali uweze kuwa nami usiku huu”

Nikakaa kimya kwa sekunde kadhaa huku nikimdadisi Halima machoni mwake. Manzi huyu wa kikenya kwa kweli ni mashine, kwani ana vigezo vyote vya kuwa msichana anaye tamanisha.

“Tafafhali nina kuomba. Nina ona una pete ya kidoleni na nilisikia ukizungumza na mke wako, ila nina kuomba sana kwa usiku wa leo unipe kampani ya kuwa nami”

“Poa usijali, nita lala hapa kwenye kochi”

“Nashukuru sana”

Halima akachukua taulo na kuingia bafuni, nikasikia maji yakimwagika ikiashiria kwamba ana oga. Nikatoa bastola zangu mbili na kuzitoa magazine zote na kuziweka kwenye mfuko wa koti. Kisha kila bastola nika irudishia sehemu yake. Baada ya dakika kumi Halima akatoka akiwa amejifunga taulo lililo ufanya mwili wake wa umbo namba nane kuonekana vizuri. Makalio yake makubwa na yaliyo nona yakanifanya nizidi kumtamani. Akapanda kitandani huku kitaulo chake kwa dakika kadhaa kikiyaacha mapaja yake wazi. Akawasha tv kishaa akazima taa ya chumbani hapa na mwanga huu wa tv una nifanya niweze kuona jinsi mitego yake anayo nipatia kitandani hapa.

‘Eddy una mke tulia’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikimshika na kumminya jogoo wangu ambaye tayari amesha simama kisawa sawa.

“Huumii hapo kwenye sofa?”

“Hapana”

“Kama una umia njoo hapa kitandani”

“Nina shukuru”

Nilijibu kujikaza tu ili shetani wa mapenzi asinitawale.

“Mmmm hii A/C mbona ina toa upepo mdogo?”

Halima alizungumza hukua kichika rimoti ya A/C akaminya minya na kuongeza upepo unao endelea kutawala ndani hapa. Halima akazidi kwenda mbali, akalala kifudi fudi, na kufanya makalio yake kukaa kama kichuguu chenye mteremko mkali sana.

‘Kukicha salama leo, kweli mimi mwanaume’

Niliendelea kujifariji, ili kuzidi kumpotezea Halima na nisizidi kumtamani, nikatoa simu yangu mfukoni na kuanza kucheza game ya mapigano. Baada ya dakika tano Halima akawasha taa na kunitazama. Akashuka kitandani huku macho yakiwa yamemlegea.

“Eddy najua sio vizuri kwa mwanaumke kumtamkia mwanaume kwamba nina hitaji penzi lake. Eddy nikiwa nina hasira au kwenye huzuni huwa nina penda nitombw** hadi nirudi kwenye hali yangu ya kawaida”

“Heee!!”

Niliduwaa na tayari Halima akawa amesha livua taulo na kubaki kama alivyo zaliwa. Akapiga magoti mbele yangu na kunishika kifungo cha suruali yangu na kukifungua, akanifungua zipu na kuingiza kiganja chake ndani ya suruali yangu na kumtoa jogoo wangua mbaye tayari amesha simama wima. Akaanza kumnyonya na kunifanya nianze kutoa miguno ya kimahaba. Nikavua koti langu la suti, nikaliweka pembeni, bastola zangu mbili nikaziweka pembeni. Nikavua shati na Halima akamalizia kunivua suruali na boksa. Mtoto huyu wa kike akazidi kunionyesha maujuzi yake ya kunyonya jogoo. Ila katika vitendo vyake hivyo sikuhitaji kujipumbaza kwani siwezi kumuamini kwani ana weza kufanya jambo lolote la kunidhuru. Alipo hakikisha amejiridhisha, akanikalia mapajani mwangu huku taratibu akimkalia jogoo wangu. Halima akazidi kuniburudisha kiasi cha kunifanya nijisikie furaha. Nikamnyanyua na nikasimama huku nikiwa nime mbebe na kuendelea umpatia burudani isiyo ya kawaida. Kama alivyo dai kwamba ana hitaji kushuhulikiwa kisawa sawa ndivyo jinsi nami nilivyo hakikisha kwamba nina mshuhulikia kisawa sawa hadi akafika kileleni mara mbili mfululizo nani ndipo nikamaliza mzunguko wa kwanza kwa upande wangu.

“Ehee aisee wewe nikiboko, sijawahi kupelekeshwa hivi na kufika kileleni mara mbili mfululizo”

“Upo Tanzania haupo Kenya mama”

“Haki ya Mungu mke wako ana faidi”

“Eti ehee?”

“Ndio, yaani ume nifanya leo nijisikie kitu cha tofauti sana kwenye mapenzi. Hongera sana Eddy”

“Nashukuru”

Nikashuka kitandani na kuingia bafuni, nikaoga haraka haraka na nikarudi chumbani. Sikulala zaidi ya kukaa kwenye sofa hadi kukapambazuka. Majira ya saa mbili asubuhi tukatoka hotelini hapa na moja kwa moja nikampeleka Halima hadi katika duka la bwana Selemani Selemani.

“Samahani Eddy hujanipatia namba yako ya simu, siku nikija Tanzania, niweze kukutafuta tena”

Nikmatajia Halima namba yangu ya simu kisha naye akanitajia namba yake ya simu kisha akashuka kwenye gari na kuondoka. Nikaondoka na breki ya kwanza ikawa ni getini kwangu, nikaacha gari nje ya geti kwa maana sikai sana ndani kwangu. Nikaikagua nyumba yangu kama kawaida yangu na nikaridhika. Nikaoga na kubadilisha nguo hizi nilizo zivaa, nikavalia kaunzu pamoja na kofia yake na kobazi kisha nikarudi kwenye gari na kuanza safari ya kuelekea ukweni. Nikiwa njiani simu yangu ikaanza kuita huku namba inayo ingia ni private. Kidogo nikastuka, nikasimamisha gari pembezoni mwa barabara kisha nikaipokea simu hii.

“Halooo Eddy. Umewaua vijana wangu ume tafuta bifu ambalo nina kuahidi ni lazima nita kuuaa.”

Sauti nzito ambayo kwa utaalamu wangu nina tambua sio ya mtu halisi anaye zungumza, niliisikia vizuri masikoni mwangu.

“Ohooo una jua siku zote ukiwa na adui yako ni bora kuzungumza na sauti yako halisi. Usitumie voice changer ukahisi nita kuogopa. Kabla ya kuniua nita kuua wewe kwa maana ninakujua A to Z kama ulisha wahi kuchezea wajinga wengine basi nikutabiri kifo kwmaba ume ingia choo cha majambazi tena wenye uchu ikiwa wewe ni mwanamke mwenye bikra ya mbele ya nyuma. So jiandae kufa kenge wewe”

Nilizungumza kwa kujiamini sana.

“Hahahahahahahaa.a……ahaha. Eddy Eddy Eddy Eddy. Najua hunijiu vizuri.”

“Oya acha ukum** kama ni mwanaume kweli njoo nifwate alafu ujue nipo vipi. Alafu tusiharibiane siku nime vaa vazi la heshima”

Nikakata simu na kuendelea na safari yangu huku mapigo yangu ya moyo yakinienda kasi sana kwa maana nimesha vurugwa moyoni mwangu. Nikafika katika geti la wake zangu, nikapiga honi moja na geti likafunguliwa, nikasimamisha gari eneo la maegesho na nikashuka. Mdogo wa Cauther wa kike akanipokea na kunisalimia kwa heshima kubwa sana. Nikawasalimia ndugu wote nilio wakuta hapa.

“Cauther yupo wapi?”

“Yupo chumba cha maandalizi, huko ana fundwa na makungwi, hivyo haruhusiwi kuongea na simu wala wewe kumuona hadi siku ya harusi?”

Nadia mdogo wa Cauther aliniambia huku akinitazama usoni mwangu.

“Duuu kwa hiyo hadi kesho?”

“Ndio shem”

“Baba yupo wapi?”

“Baba ametoka asubuhi hii pamoja na baba mdogo na babu. Sifahamu wamekwenda wapi?”

“Sasa nifanyie basi mpango niisikie sauti yake tu “

Nadia akaninyooshea kiganja cha mkono wake wa kulia ikiwa ni ishara ya kuomba kitu. Nikajiongeza kwa haraka na kutambua ana hitaji pesa. Nikatoa elfu hamsini katika wallet yangu na kumkabidhi, akatingisha kichwa ikiwa ni ishara ya kwamba haitoshi.

“Basi nina kuingizia kwenye simu kwa maana sija tembea na Cash nyingi”

“Sawa ila sifanyi kazi yako hadi unipe kiasi cha kutosha”

Nikamuingizia kiasi cha laki mbili katika simu yake, akatabasamu kisha akanisogelea na kuninong;oneza.

“Nenda kwenye gari lako kwa maana nita kupigia video call umuone kidunchuuu tu kisha baada ya hapa nina kata”

“Sawa shem”

Nilizungumza kwa kutabasamu kwa maana katika ndugu wa Cauther ambao hapo awali kidogo walikuwa wana nielewa na kunipenda ni Nadia sema alipo kuwa na ndugu wengine tofauti na Cauther ilikuwa ina mbidi kunichukia. Nikatoka nje na kuingia ndani ya gari langu, hazikuisha hata dakika mbili Nadia akanipigia whatsapp video call.

“Hei shem dakika moja tu una ongea naye”

“Sawa”

Nadia akamkabidhi Cauther simu, nikamuona jinsi alivyo pambwa.

“Waooo ni wewe?”

Cauther akatabasamu,

“Ni mimi mume wangu, simu hapa nimepokonywa jana usiku na bibi. Yaani wee acha, hapa siruhusiwi hata kutoka nje kuonana na watu, ni ndani na mimi”

“Pole mke wangu, ila una jisikiaje?”

“Nina jisikia vizuri mume wangu. Nina hamu sana na wewe”

“Dakika moja moja ime kwisha. Shem kama una taka kuongea naye kwa dakika moja nyingine ongeza dau”

Nadia alizungumza huku akiwa amempokonya simu Cauther.

“Nadia usinifanyie hivyo bwanaa”

Cauther alilalama.

“Shem ni wewe, au nikate simu”

“Basi nina kuingizia tena”

“Niingizie ndio nimpe”

Ikabidi nimuingizie tena laki mbili na nusu ndipo akamkabidhi Cauther simu.

“Ehee baby vipi umesha jiandaa?”

“Mimi nipo tayari mke wangu, nilisha waambia washakaji juu ya harusi yangu, kesho kina Maulid na Judy nao wata kuwepo”

“Waooo nita furahi sana mume wangu”

“Usijali nina kupenda sana mke wangu”

“Nina kupenda pia mke wangu. Alafu hiyo kanzu na barakashia vimekupendeza sana”

“Kweli?”

“Haki ya Mungu vime mupendeza sana”

“Nashukuru mke wangu”

“Nawapa dakika moja ya ofa”

Niliisikia sauti ya Nadia akizungumza.

“Hahaa shem una vituko sana. Vipi wewe harusi yako lini?”

“Mimi bado bado, malizeni kwanza nyinyi kisha mimi nita fwata”

“Haya bwana. Ehee mke wangu kesho asuhuhi na mapema nita fika hapa”

“Sawa mume wangu. Kuwa makini sana, si una jua sina simu na kama ni simu ni hadi niibe hivi ya Dogo ndio tutakuwa tuna zungumza”

“Ahaa sawa mke wangu”

Cauther akanibusu kisha akamkabidhi Nadia simu yake.

“Shem baadae na shukrani”

“Poa shemeji, alafu hujakunywa chai”

“Muda umesha kwenda”

“Sawa hakikisha una pendeza siku ya harusi”

“Usijali kama kawaida nita pendeza”

“Sawa shemeji yangu”

Nikakata simu na kuondoka nyumbani hapa. Nikapita katika kijiwe changu cha kuendesha taksi na kuwasabahi waskaji wangu na kuwaeleza juu ya harusi yangu hii ambayo upande wa familia wameamua kuifanya ili kuiridhisha mioyo yao kwa maana nilimuao Cauther kwa dini yangu ya kikristo. Waskaji wangu wakajawa na furaha na wakaniadi wataandamana nami kwenye sherehe hiyo. Nikaondoka na moja kwa moja nikaelekea nyumbani kwa Willy.

“Dogo kuna fala mmoja amenipigia kwa private namba. Je tuna weza kuitrack namba na kufahamu ni nani?”

Nilizungumza mara baada ya kusalimiana na Willy.

“Ina wezekana”

“Alafu bwege ametimie voice changer”

“Nashisi ni mtu ambaye una mjua ndio maana ameamua kubadilisha simu. Eheee jana ulifahamu ni namba ya nani?”

“Mwnamake wa jaaa niliye muua na wezake, alidai kwamba alimsikia bwana wake kwamba ana zungumza na mtu na alipo muuliza akadai ni makamu wa raisi hivyo hajui ni makamu wa raisi wa nchi gani?”

“Duuu broo hili limesha kuwa ni kisanga kwa maana si unajua mkulu umesema ume mkoromea na kukataa kazi yake, sasa ni laizma ata kuwinda ili kukumaliza”

“Ndio maana nina kuwa makini sana mdogo wangu. Alafu nina hitaji kuwasiliana na rafiki zangu wanne wa Japani, nina hitaji kuwapatia kazi moja hivi. Hivyo nitahitaji kutumia computer yako kuwasiliana nao kwa maana mawasiliano yetu ni ya code. So laptop yako si hakuna anaye weza kuitrack?”

“Looo!! Kaka hakuna anaye weza kuingia kwenye sever zangu labda Mungu tu ndio anaye weza kujua niacho kifanya kwenye laptop yangu.”

“Hapo sawa kaka”

Nikamuelekeza Willy jinsi ya kuwasiliana na rafiki zangu hao wanne ambao ni kati ya maninja hatari sana nchini Japani. Baada ya dakika kumi wote nikawa katika mazungumzo ya video call.

“Habari zenu ndugu zangu”

Nilizungumza kwa lugha ya Kijapani na kumfanya Willy kunitumbulia macho ya mshangao.

“Salama X pole kwa kuwapoteza rafiki zetu. Tulipokea habari za misiba yao kwa uchungu sana na tulipo gundua kwamba wewe upoa hai tukajawa na imani kwamba ipo siku tu uta tutafuta. Tuna shukuru kwa kufanya hivyo”

Mmoja wao alinijibu kwa kijapani.

“Asanteni. Nina kazi moja nina omba tuweze kusaidiana.”

“Kazi gani X”

Nikawaleza mpango wangu mzima wa jinsi nitakavyo kuwa katika ulinzi wa raisi nchini Ujerumani. Nikawalezea hali nzima ya kundi la Scropion kuanzia kiongozi wao, hadi mtu wa nafasi ya chini. Kila kitu nilicho kiona kwenye flash aliyo nipatia baba mkwe nika nikawaleza kwa maana ni watu nina waamini.

“Basi tukikutana Ujerumani tuta kusaidia kwa kila jambo na walio husika kwenye vifo vya rafiki zetu ni lazima tuwaondoe mmoja baada ya mwengine.”

“Nina washukuru sana rafiki zangu.”

“Sisi ni makaka na tuliapa udungu wetu kwa kunywa damu zetu wenyewe. Hivyo hatuta kubali kukuona ndugu tetu una pata shida na sisi tukakaa pembeni, sisi ni wamoja na hakuna atakaye tutenganisha hadi kifo”

“Asanteni sana”

“Nashukuru”

Tukamaliza mawasiliano na nikakata simu, nikamgeukia Willy.

“Broo wewe kiboko, yaani toka ulipo anza kuzungumza hadi una maliza sija kunyaka hata jambo moja”

“Hahaaa ni ngumu sana kukijua kijapani, tena kila cha ndani kabisa”

“Duuu, hao ni kina nani?”

“Ndugu zangu hawa ndio walio nifundisha mimi kuwa ni ninja, so kama nilivyo waambia kuna manja wameandaliwa kwa ajili ya kumuua raisi, hivyo sio rahisi kupambana nao nikiwa peke yangu kwani ninao ambata nao sio maninja ni walinzi wa kawaida tu. Hivyo nina hofia maisha yao kufa”

“Duu ina bidi wawe makini sana?”

“Zaidi ya umakini. Ehee ume pata kujua namba ya nani?”

Willy akanijibu kwa kuminya start batani ya keybord ya computer yake. Ikaja picha ya makamu wa raisi na yeye ndio mtu ambaye amenipigia simu hiyo kwa maana Willy ameyachuja mazungumzo ya sauti hiyo hadi ikabaki sauti ya makamu wa raisi kwa maana kila simu inayo ingia kwenye simu yangu huwa ina rekodiwa automanical katika simu yangu.

“Willy”

“Ndio kaka”

“Usiku wa leo nina kwenda kumshikisha adubu huyu mzee. Kesho akiamka ata kuwa na akili mpya. Nikimuacha hivi ata kuwa kama mwanamke wa uswahilini anaye niimbia imbia mafumbo ya taarabu. Sasa ili kumuonyesha kwamba mimi ni mshenzi nina kwenda katika muonekano wangu wa kininja na asipo kuwa makini, nina muua”

Nilizungumza kwa msisitizo huku nikikiitazama picha ya makamu wa raisi kwenye kioo kikubwa cha computer hii hadi Willy akajawa na wasiwasi mwingi sana kwa maana roho ya kikatili imesha nitawala moyoni mwangu.



“Broo”

Willy aliniita kwa woga kidogo huku akinitazama usoni mwangu.

“Ahaa kama unavyo jua makamu wa raisi ana mtandao mkubwa na ana nguvu kuwa hapa nchini. Ita kuwaje kama akikushika au akwa amefanya hivi kwa ajili ya kukumpima na kukuona uta fanya nini. Una onaje tukaachana naye kwa sasa”

Willy alizungumza kwa sauti ya unyenyekevu.

“Simuui ila nina mfundisha adubu”

“Ila kaka ukifanya hivyo uta kuwa ume haribu ita kuwaje kama ukipata madhara ikiwa kesho tu ni harusi yako ya pili”

“Hakuan atakaye weza kunidhuru”

“Broo, kumbuka shemeji ana kuhitaji kesho. Hembu tumuache shetani huyu apite ila kesho ukamilishe kile cha kukamilisha alafu hawa watu udili nao kivingine. Tafadhali kaka nina kuomba”

Nikashusha pumzi nyingi huku nikiutafakari ushauri huu wa Willy, ukiangalia ni kweli, endapo nitapata madhara kesho sinto weza kumuoa Cauther na nita kuwa nime muharibia sana mipango yake.

“Sawa nime kuelewa”

Simu yangu ikaingia ujumbe wa meseji, nikaufungua na kukuta ni kutoka kwa raisi.

“Njoo ikulu”

Nikautazama kwa sekunde kadhaa. Kisha nikampigia simu, simu ikaita kisha ikapokelewa.

“Ndio muheshimiwa”

“Nina imani kwamba ume upata ujumbe wangu?”

“Ndio mkuu”

“Karibu”

“Sawa”

Nikakata simu huku nikimtazama Willy usoni mwake.

“Nina kwenda ikulu mara moja”

“Ila kaka nina kuomba sana ushauri wangu uweze kuufanyia kazi. Kesho tuna hitaji tule ubwabwa kwa amani”

“Poa mdogo wangu. Ila hakikisha kwamba una fwatilia nyendo za makamu wa raisi. Hususani kwenye namba zake”

“Sawa”

Nikaondoka nyumbani kwa Willy na moja kwa moja kuelekea ikulu. Nikasimamisha gari langu eneo la magesho lililopo hapa ikulu, nikaelekea ofisini kwa raisi.

“Ingia Eddy”

Raisi alizungumza mara baada ya kuniona nime simama mlangoni mwa ofisi yake huku mlango huo ukiwa wazi kidogo. Nikaingia huku nikiurudishia mlango, nikaka kwenye kiti kilichopo mbele ya ofisi yake.

“Naona ume toka kwenye vazi la kishehe au ndio maandalizi ya harusi nini?”

“Hahaa ndio muheshimiwa”

“Hongera sana, huko ndio kukua”

“Nashukuru ila nina funga naye mara ya pili kwa maana nilifunga naye ndoa ya kikristo na wazazi wake wameamua nifunge nao kwa ndoa mila zao za kiarabu”

“Ahaa sawa sawa. Baba yake alikuwa hapa, akanipa mualiko huo niweze kuudhuria ndoa ya mwanaye”

“Ina maana una mfahamu yule mzee?”

“Yaa ni mfanya biashara mmoja wapo kati ya wale walio wekeza pesa zako katika kipindi cha uchaguzi hadi nika ingia ikulu”

“Ahaa vipi lakini uta kuwepo kwenye harusi yangu?”

“Ahaa kwa kesho kusema kweli ratiba yangu ime bana.”

“Hakuna shaka muheshimiwa”

“Jamboa ambalo nilihitaji kukueleza ni kwamba ule mpango umesha kamilika na nina ona Msuya ameweza kumudu kila kitu kwangu hadi mke wangu ameshangaa”

“Yaa nilipo mchagua yeye nilitambua wazi kwamba ni lazima aweze kumudu kazi hiyo”

“Ehee nipatie mpango wako mzima wa ulinzi siku ya mkutano?”

“Mpango bado sijapanga ila nikipanga nita kuambia au utajionea siku ikifika”

“Ahaa sawa, hakuna shaka. Endapo mwenyezi Mungu akiturudisha salama, nime kuandalia mapumziko yako na mke wako, muende nchini Brazil, hivyo kama ni hoteli ya kwenda kukaa kule uta niambia ni ipi ili tuweze kuweka booking mapema”

“Waooo asante sana muheshimiwa”

“Nashukuru nawe pia kwa kuwa nami. Kumbuka kwamba wewe ndio mtu pekee ninaye kuamini kwenye hii nchi.”

“Hakuna shaka muheshimiwa ila tukiwa Ujerumani nita kupa majina ya watu wanao paswa kuondolewa kwenye hii serikali”

“Hakuna shaka Eddy”

“Okay je kuna la ziada?”

“Hapana”

“Nashukuru”

Nikanyanyuka kabla sijatoka raisi akaniita.

“Ndio muhehsimiwa”

“Eddy nina swali nina omba nikuulize?”

“Sawa mkuu”

“Ume achia nafasi kubwa sana katika jeshi. Ilikuwa bado nafasi moja uwe mkuu wa majeshi. Una onaje uka rudi kwenye nafasi yako na ukirudi nikupandishe uwe jenerali wa jeshi kabisa na sio Luteni Jenerali. Nina imani ukiingia jeshini nchi itakuwa na nguvu, tuta kuwa na uwezo wa kuwaondoa maadui zetu, iwe watek au wasitake?”

Nikashusha pumzi kidogo huku nikimtazama raisi machoni mwake.

“Nina hitaji nikiondoka kwenye kiti chako au chochote kikitokea kwenye maisha yangu uje kuishika nchi”

“Ila mkuu mbona sija fikiria kabisa kuwa kiongozi wa hii nchi. Napenda kuwa mimi kama mimi, nina penda kuishi maisha ya kawaida”

“Najua hilo Eddy, ila kama unavyo fahamu nimesha poteza nguvu”

“Ila huko kwenye majeshi najua wata kuwa wana muunga mkono huyu jenerali wa sasa ambaye yupo bega kwa began a makamu wa raisi”

Raisi akavua miwani yake na kuiweka mezani.

“Eddy”

“Naam”

“Nahitaji kujifanya mjinga, nahitaji tusaidiane kumtoa adui yetu taratibu”

“Ngoja kwanza mkuu, nina ona una zungumza kuhusiana na adui adui. Je una mjua?”

“Ndio nina mjua”

“Ni nani?”

“Ni makamu wangu wa raisi”

“Umejua toka lini ni adui yako?”

“Siku nyingi sana Eddy, japo siku ile nilikupa lile faili ili kukupa changamoto za kumtafuta nani ni adui kamili kwa maana nina ujua uhusiano wako wewe na makamu wa raisi ni kama baba na mwana hivyo ingekuwa ni ngumu kwa mimi kukueleza moja kwa moja kwamba adui yangu ni makamu wa raisi, ungehisi kama nina kuchonganisha”

“Nime kuelwa mkuu, acha kwanza twende Ujerumani na kurudi, hayo mengine yatafwata”

“Sawa Eddy nashukuru kwa muda wako”

“Asante”

Nikaondoka ikulu hapa huku akilia yangu ikipanga na kupangua nini nifanye kuhakikisha kwamba nina weza kuvuruga utawala wa makamu wa raisi. Nikaopokea simu yangu ninayo pigiwa na Judy

“Kaka kwema”

“Kwema mdogo wangu”

“Kwema kaka tu. Vipi upo wapi?”

“Natola ikulu, nina kwenda home kupumzika”

“Ehee kesho sherehe saa ngapi?”

“Muje nyumbani hapa saa mbili asubuhi, kisha kama saa nne hivi tuta elekea kule”

“Sawa kaka ni hilo tu nilihitaji kulifahamu”

“Poa dogo”

Nikakata simu na moja kwa moja nikaelekea Bagamoyo katika nyumba yangu ya siri. Nikaingia katika chumba changu cha siri ambacho nina hifadhia nguo za kininja pamoja na silaha zake. Nikafungua moja ya sanduku kubwa la mbao na nikazitazama nguo za jeshi za kijana kilicho kolea ambazo zina vyeo meja jenerali. Nikavua nguo zangu hizi na kuzivaa nguo hizi pamoja na kofia yake. Nikasimama mbele ua kioo kikubwa kilichopo ndani hapa.

‘Eddy rudi kazini’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikiendelea kujitazama kuanzia chini hadi chini. Katika kuzivaa nguo hizi hii ni mara ya pili kuzivaa, mara ya kwanza ni siku ambayo nilikuwa ninapandishwa cheo na kuwa Luteni jenerali wa jeshi, na baada ya hapo sikuweza kuzivaa kwa maana niliendelea kutekeleza majukumu ya kawaida katika kikosi changu cha X.

‘Muda sahihi wa kurudi jeshini bado’

Nilizungumza huku nikikanza kuvua shati hilo. Nikavaa nguo zangu za kawaida, nikatoka katika chumba hichi na kuingia katika chumba kingine, nikazitazama picha kadhaa ambazo nilipiga na marafiki zangu ambao kwa sasa ni marehemu. Nikawasha mishuu maa mwili, na nikawaombea wezangu hawa, kisha nikarudi nyumbani kwangu jijini Dar es Salaam. Sikuhitaji kuelekea sehemu nyingine yoyote zaidi kukaa nyumbani kwangu.

Asubuhi na mapema nikajiandaa. Maulid na Judy wakafika nyumbani kwangu, nikavaa vazi langu la harusi na kuondoka nyumbani kwangu hapa huku tukitumia gari la Judy.

“Tupitieni kijiweni kwangu nikawapitie waskaji wangu”

“Poa kaka”

Tukapita katika kituo cha waendesha taksi wezangu na kuwakuta wakitusubiria. Msafara wa kuelekea ukweni ukaanza huku washkaji wangu wakiwa wametengeneza msafara mkubwa sana. Tukafika kwa wakwe zangu na kupokelewa vizuri. Maulid ndio mpambe wangu kwa upande wangu.

“Karibuni sana”

Shemeji yangu alinikaribisha.

“Nashukuru sana”

Tukaonyeshwa eneo la kukaa.

“Kaka hawa raia wana pesa sana”

Maulid alininong’oneza.

“Yaa wana pesa nyingi sana”

Tukapata chakula huku tukisubiria muda wa kufunga ndoa ufike. Makamu wa raisi na walinzi wake wakafika eneo hilo.

“Shikamoo mzee”

“Marahaba, hongera sana”

“Nashukuru sana mzee”

Makamu wa raisi akaka katika eneo ambalo ameandaliwa. Shuhuli zikaanza huku kukiwa na baadhi ya dua zikisomwa kisha ukafika wakati wa kufunga ndoa. Tukafwata kanuni zote za kiarabu katika kumuoa Cauther na nikakabidhiwa rasmi kuwa mke wangu. Sherehe zikaendelea huku watu wakila na kunywa.

“Umependeza mke wangu”

“Nashukuru hata wewe umependeza mume wangu. Nina shukuru sana kwa kuwa na mimi”

“Wewe ndio napaswa kukushukuru”

Judy akatufwata sehemu tulipo kaa na kuninong’oneza.

“Mkuu kuna hii picha hapa Willy amenitumia kwenye simu yangu”

Judy akanionyesha picha ya jamaa mmoja ambaye nina mfahamu ni mmoja kati ya magaidi ambao walimteka raisi.

“Anadai kwamba wapo hili eneo”

Mapigo yangu ya moyo yakanienda kasi huku taa nyekundu ya hatari ikiwaka kichwani mwangu.

“Ume waona?”


ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

BLOG