Search This Blog

Wednesday, November 18, 2020

POWER SEHEMU YA 1/10

 


 POWER

WRITER…………………………………………EDDAZARIA G.MSULWA
WEBSITE………………………………………… www.storyzaeddytz.com
CONTACT……………………………………….. 0657072588/0768516188
AGE……………..18+ 

SEHEMU YA 1 KATI YA 10

 


Mama kwa haraka akaniziba mdomo wangu huku tukiwa tumejibanza kwenye migomba mingi sana, iliyopo karibu kwenye kijumba chetu cha udongo huku tukimshuhudia baba akipigwa kipigo na watu walio valia mavazi meusi huku wakiwa wamezificha sura zao kwa vitambaa. Bariki kali na mvua kubwa inayo endelea kunyesha katika eneo hili la kijiji chetu cha Umbwe hapa Moshi, ikamfanya mama azidi kunikumbatia huku akilia kwa sauti ya chini chini sana. Machozi na hasira zikazidi kunitawala, ila sina uwezo wa kufanya kitu chochote nikiwa bado ni mtoto mdogo mwenye umri wa miaka sita.

“Wewe si unajifanya mjanja kuwashawishi wakulima wezako kukataa mimi kuwekeza kwenye hichi kijiji si ndio?”

Sauti ya mwanaume aliye zungukwa na watu hawa wanao endelea kumtesa baba ilisikika vizuri, japo mama alijitahidi kuniziba macho yangu nisishuhudie kitendo hicho anacho fanyiwa baba yangu, ila nikazidi kujitahidi kuangalia ila mama aliigeuza sura yangu pembeni na nikaendelea kunikumbatia. Niliendelea kusikia miguno ya baba yangu na kilio chake cha maumivu.

“Sasa utakufa kama shujaa mpuuzi, mpigeni hadi afe na mwili wake mukautupe shambani kwake”

Sauti ya mwaunaume huyo iliyoa maagizo hayo na kuwafanya watu hao kuendelea kumpiga baba kwa magongo mazito. Kwa bahati mbaya ikapiga radi mwanga wake ukaangaza kila eneo hili.

“Kuna watu kule kwenye migomba”

Kijana mmoja alizungumza huku akinyoosha mkono wake kwenye eneo hili tulilo jificha na mama. Kwa haraka mama akanishika mkono wangu wa kuli na hapakuwa na budi tena zaidi ya kuanza kukimbia.

“Lole kimbia”

Mama alizungumza huku akiniachia mkono na kuanza kuchechemea.

“Ndefo mama”(Mama twende)

Nilizungumza kwa lugha ya kichaga huku nikijaribu kumshika mkono mama ila mama kwa ishara akaniomba nikimbie kwani watu hao wanazidi kutukaribia. Machozi ya yakazidi kunimwagika usoni mwangu, kwani sina uwezo wa kupambana na wanaume hawa na wala sina uwezo wa kumtetea mama yangu. Mama kwa ishara ya mkono akazidi kunisisitizia niweze kukimbia ili kuyaokoa maisha yangu.

Nikakimbia kwenye hii migomba mingi, huku nyuma nikaanza kusikia sauti ya mama yangu akipiga mayowe ya kuomba msaada. Ila mvua na mingurumo hii ya radi na umbali tulipo kutoka jirani mmoja hadi mwengine ni swala ambalo ni gumu sana kusikika. Kila nilipo jaribu kusonga mbele, nikajikuta nikisita kabisa kuendelea na safari hii. Nikaangaza angaza chini na kuona fimbo, nikaichukua na kuanza kurudi eneo nilipo muacha mama yangu huku machozi yakinimwagika usoni mwangu na hasira ikiwa imejaa kifuani mwangu.

Nikafika katika eneo ambalo yupo mama yangu, nikawakuta vijana hawa sita wakimbaka kwa nguvu, jambo lillo nifanya nianza kumchapa mmoja wao.

“Ametokea wapi huyo mtoto”

Kijana mmoja ambaye ndio yupo katikati ya mapaja ya mama alizungumza huku akiwa amevua kitambaa kilicho kuwa kimeiziba sura yake.

“Mpigeni”

“Mkuu ila huyu ni mtoto”

“Mtoto mpigeni na mumuue”

“Ja….ma…..ni….musi….mp……”

Mama alizungumza kwa shida sana kwani amepigwa kipigo kizito sana na kubwa juu.

“Muondoeni hapa”

Kijana huyo anaye endelea kumuingilia mama kinguvu alizungumza na vijana wake wawili wakanishika na kunibebe juu juu. Nikajitahidi kwa nguvu zangu zote ili mradi niweze kujitoa mikononi mwao na kwenda kumsaidia mama ila utoto wangu na kuto kuwa na nguvu, ukawafanya vijana hawa kunihimili. Vijana hawa wakaendelea kunibeba huku wakinitandika magofi mazito pamoja na ngumi katika kila sehemu ya mwili wangu.

“Tumuue”

Kijana mmoja alizungumza kwa ukali huku wakinibwaga chini kama mzigo wa kuni.

“Hapana huyu ni mtoto mdogo sana, hatuna haja ya kumuua”

“Tumepewa agizo na mkuu?”

“Ni bora tumtupe huko kwenye korongo, akafie mtoni”

Niliweza kuyasikia mazungumzo ya vijana hawa vizuri sana, ila uwezo wa kusimama sina kwa maana wamenipiga sana ngumi na makofi kana kwamba wana mpiga mtu mzima mwenzao. Wakanisukumia bondeni kwenye korongo kubwa na nikaanza kumbingirika huku nikipia kelele za kuomba msaada, ila galfa nikahisi kishindo kikubwa kichwani mwangu na taratibu macho yangu yakapoteza uwezo wa kuona na sikujua ni nini kinacho endelea.

***

Nikaanza kusikia sauti ya watu wawili wakizungumza huku mmoja akiwa ni mwanamke. Sauti ninazisikia ila kile wanacho kizungumza kwangu ndio mtihadi kabisa kwani ni lugha ambayo siifahamu. Nikafumbua macho yangua, taratibu ila ukungua mwingi ulio yatawala macho yangu ukanifanya nisiweze kuona watu hao.

“Heii boy”

Niliisikia sauti ya kike ikizungumza pembeni yangu.

“Ameamka”

“Unajisikiaje kijana?”

Watu hawa waliendelea kuniuliza maswali ambayo sikuweza kuyajibu kwa maana siwaoni vizuri.

“Unaweza kuzungumza?”

Mwanamke aliniuliza kwa sauti ya upole.

“Tumuache apumzike kwa muda ndio tumulize maswali”

“Ila ni kijana mzuri sana”

“Yaa sijui ni kwa nini waswahili wanawanyanyasa watoto hivi”

Nikajaribu kumtazama mwanaume huyu, taratibu nikaanza kuiona sura yake, ni mzee wa kizungu mwenye mvi nyingi sana kichwani mwake. Nikamtazama mwanamke aliye simama pembeni ya mzee huyu, naye ni bibi wa kizungu, ila hajazeeka sana kama huyu mzee.

“Mtengenezee supu nzuri ya kuku”

Mzee huyu alizungumza, bibi huyo akambusu mumewe shavuni kisha wakatoka ndani hapa. Mzee huyu akavuta stuli na kukaa pembeni ya hichi kitanda. Akaanza kunishika shika mguu wangu wa kushoto, taratibu nikautazama mguu wangu na kujiona nikiwa nimefungwa bandeji kwenye mguu mzima. Nikaanza kulia, kwa maumivu niliyo anza kuyahisi mara tu ya kuuona mguu wangu.

“Hapana kijana usilie”

“Nipo wapi…...?”

Niliendelea kulia huku nikijitahidi kukaa kitandanii. Mzee huyu akajitahidi na kunirudisha na kulala. Maumivu ya kichwa nayo yakazidi kunichanganya. Mzee huyu akachukua moja ya bomba la sindano lenye dawa na kunichoma mkononi mwangu. Taratibu nikaanza kuhisi usingizi ulio nifanya nilale fofofo ndani ya muda mchache tu.

***

Baada ya siku mbili nikapata nafuu kidogo hata ya kuka mwenyewe kitandani, mzee Klopp na mke wake Bi Jane Klopp, kama walivyo jitambuisha jana, wakaniomba waweze kuzungumza na mimi. Kwa haraka haraka katika kipindi hichi cha siku hizi mbili nilizo kaa nao wamekuwa ni watu wa kunijali kwa kila jambo. Muda wao mwingi wanautumia katika kunitazama na kujua hali yangu inaendeleaje.

“Unaitwa nani?”

Bi Jane Klopp aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.

“Eheee?”

“Unaitwa nani?”

Nikajaribu kukumbuka jina langu, ila nikajikuta nikishindwa kulikumbuka kabisa.

“Je unajua ni nini kimekukuta?”

Bi Jane Klopp aliendelea kuniuliza kwa upole, ila nikashindwa kabisa kufahamu ni kitu gania mbacho kimenipata.

“Hapana, kwani nipo wapi?”

Niliuliza kwa suati ya upole na unyonge.

“Upo Arusha mjini”

“Nimefikaje fikaje?”

Bibi Jane Klop wakatazamana na mume wake huku wakionekana kujawa na mshangao sana.

“Okay, siku chache zilizo pita tulikuwa Moshi, kwenye matembezi yetu ya kufanya uchunguzi ulio tuleta huku nchini Tanzania, kwa bahati nzuri tuliweza kukuta kwenye moja ya mto ukiwa umepoteza fahamu, ilikuwa ni alfajiri sana.”

Mzee Klop alizungumza kwa upole huku akinitazama usoni mwangu.

“Tulipo kuchunguza vizuri tukagundua kwamba upo hai, tukaona sio mbaya tukakusaidia kwa maana bado ni mtoto mdogo sana”

“Asanteni”

“Usijali, ni jukumu letu. Je unakumbuka kama una ndugu, au marafiki ambao tunaweza kuwasiliana nao wakaja kukuchukua hapa?”

Nikatingisha kichwa huku nikijitahidi kuvuta japo taswira ya mtu yoyote ninaye mfahamu kwenye maisha yangu ila sikuweza kukumbuka. Kitu kilichopo hapa kichwani mwangu ni hawa wazee wawili mbele yangu.

“Kutokana hapa Tanzania tumebakisha muda mchache wa kukaa, basi tutafanya mpango wa kuondoka na wewe na kurudi nchini Ujerumani yalipo makazi yetu sawa”

“Sawa”

“Na kuanzia leo utaitwa Ethan Klopp, hilo ndio litakuwa ni jina lako”

“Ethan Klopp?”

“Ndio hilo ndio jina lako kuanzi hii leo”

Nikatabasamu kidogo kwani ni jina zuri kwa upande wangu na wala sioni sababu ya kukataa kulikataa kwa maana jina langu halisi silifahamu.

“Na sisi tutakuwa ni wazazi wako, kwa maana tuna binti yetu mmoja tu yupo nchini Ujerumani, na wewe utakuwa ni mtoto wetu wa pili sasa”

“Ninashukuru sana”

Nikajikuta furaha ikinitawala moyoni mwangu. Taratibu bibi Jane Klopp akanikumbatia kwa nguvu, huku akitawaliwa na furaha.

Siku zikazidi kusonga mbele huku hali yangu ikizidi kuimarika, matibabu anayo nipatia bibi Jane Klopp na mume wake yananifanya nizidi kuwa imara. Wakaanza kunifundisha vitu vingi, na wakazidi kushangazwa na uwezo wangu wa akili kwani katika kipindi cha muda mchache kila wanacho nifundisha basi ninakielewa kwa haraka na ni vigumu sana kuweza kukisahau. Wakaanza kunifundisha Kijerumani, japo ni lugha ngumu kidogo ila nikajitahidi hivyo hivyo ndani ya mwezi mzima nikawa tayari nipo vizuri kwenye lugha hiyo na hawa wakiniongelesha ninaweza kuwaelewa na kuwajibu kiufasaha.

“Ethan unajua wewe ni genius?”

Bibi Jane Ethan aliniambia tukiwa jikoni nikimsaidia kuandaa chakula cha usiku.

“Genius ndio nini?”

“Ni mtu mwenye upeo mkubwa wa kiakili, tofauti na watu wengine”

“Mtu akiwa hivyo ndio anaitwa Genius?”

“Ndio, ninakuahidi, nitahakikisha kwamba tunakupatia elimu bora unakuwa mtu bora kabisa hapa duniani”

“Nashukuru sana mama”

Bibi Ethan kama kawaida yake akainama kidogo na kunibusu kwenye paji langu la uso ikiwa ni ishara ya upendo ambao amenizoesha kuanzia siku ya kwanza kuanza kuishi nao.

“Ukiwa mkubwa Ethan unapenda kuwa nani?”

“Mmmmmm……nahitaji kuwa na nguvu?”

“Hahaaa…..hata hapo mbona una nguvu. Au unataka kuwa na nguvu ya kisiasa, kiuchumi au ushawishi katika jamii?”

“Yoyote tu ila nahitaji kuwa na nguvu tu”

“Hupendi kuwa dokta, au rubani?”

“Mmmmmmhhhh”

“Kweli?”

“Ndio mama”

“Basi kama nitaendelea kupewa maisha marefu basi nitahakikisha kwamba unakuwa na nguvu mwanangu”

“Nashukuru sana mama”

Tukaendelea kuandaa chakula hichi cha usiku, hatukuchukua muda mrefu sana tukafanikiwa kumaliza kupika, nikasaidana na bibi Klopp kutenga chakula mezani, baada ya maandalizi hayo yote kunalizika nikaelekea chumbani kumuita baba ambaye ni mzee Klopp.

“Ohooo nina kuja sasa hivi?”

“Sawa baba”

Nikaanza kuelekea mlangoni, ila kabla sijafika mlangoni akaniita, nikageuka na kumtazama, kwa ishara ya mkono akaniita na nikafika hadi kwenye kiti alicho kaa huku akiwa ana andika andika vitu kwenye kipakato chake(laptop)

“Kuna shule za primary, nilikuwa ninazitafuta hapa, nahitaji tukirudi Ujerumani uende ukasome, je ni ipi kati ya hizi mbili ni ipi hapa unaipenda?”

Mzee Klop alinonyesha majengo makubwa mawili ya shule zilizopo kwenye nchi ya Ujerumani ambapo kila siku nina tamani siku zao za kuishi hapa nchini Tanzania ziishe ili nirudi nao Ujerumani.

“Hii hapa”

Nilizungumza huku nikimuonyesha jengo moja zuri.

“Umeipenda hii?”

“Ndio baba”

“Sawa, tena hizi ni shule za watoto wenye uelewa maalumu. Tumeweza kugundua kwamba una uwezo huo”

“Nashukuru baba”

Unyenyekevu na utii ndio ngao yangu kubwa sana ya kuendelea kuishi na wazee hawa, malengo yangu na nia yangu ni kuhakisha kwamba nina pata nguvu kubwa kwenye maisha yangu, na nilazima yatime pale tu nitakapo kuwa mtu mzima. Tukatoka kwa pamoja humu chumbani na kurudi sebleni, tukapata chakula cha usiku kwa pamoja kisha tukasali ibada ya usiku kama ilivyo kuwa desturi waliyo jiwekea. Baada ya sala wao wakaelekea chumbani kwao na mimi nikaelekea chumbani kwangu na kulala.

Baada ya siku wiki tatu, kuisha, siku ya kuondoka nchi Tanzania ikawadia, kila hatua zote za kiserikali za kuondoka na mimi nchini humu walizikamilisha, japo sifahamu sana kuhusiana na mambo hayo. Tukapanda ndege ya shirika la Fast Jet hadi jijini Dar es Saalam ikiwa ndio mara yangu ya kwanza kufika katika jiji hili ambalo nilikuwa nikilisikia sikia tu kipindi cha nyuma kwamba ndio jiji zuri sana hapa nchini Tanzania.

‘Lazima nitawale hili jiji siku’

Nilijikuta nikila kiapo moyoni mwangu huku nikitazama magorofa marefu, tukiwa njiani tunaelekea katika hoteli ya karibu ili kupumzika kwa muda ili kesho asubuhi na mapema tuweze kuondoka na ndege kuelekea nchini Ujerumani. Tukafika hotelini, mzee Klopp na mkewe wakachukua chumba kimoja, huku na mimi wakinipangishia chumba changu. Baada ya kupata chakula cha usiku, tukaelelea katika vyumba vyetu ili kupumzika ili kesho alfajiri na mapema tuwe tumewasili katika uwanja wa ndege. Shauku na hamu ya kwanza ya kupanda ndege, nimesha imaliza kwa kupanda ndege kutoka Moshi hadi jijini hapa Dar es Salaam. Shauku yangu ya pili ni kwenda nchini Ujerumani kuishi kabisa. Uzuri wa mataa katika magorofa mengi ninayo yaona kwa mbali, ukanifanya muda wangu mwingi sana niutumie nikiwa nimesimama dirishani hapa nikishangaa taa hizi.

‘Nilazima uwe na nguvu ya kuawala hili jiji’

Niliisikia sauti nzito akilini mwangu iliyo nistua kidogo na kunipa wasiwasi. Damu mwili mzima ikaanza kunisisimka na vinyweleo vyangu vikaanza kusimama. Mapazia yaliyopo pembeni yangu hapa dirishani yakaanza kupepea, jambo lililo zidi kunifanya niwe na wasiwasi kwa maana madirisha ni ya vioo na yote yamefungwa vizuri sana na hakuna nafasi ya upepo kuweza kuingia na kuyafanya mapazia haya kutikisika.

‘Ethan…..Ethan…….Ethan……’

Niliisikia sauti ya kiume ikiniita kwa mbali, nikajaribu kuangaza macho yangu ndani ya chumba hichi ili niweze kuona ni nani anaye niita ndani ya hichi chumba ila sikuweza kuona zaidi ya mapazia kuendelea kutingishika sana. Woga ukanijaa, mwili mzima ukazidi kunitetemeka.

“ETHAN……..”

Sauti hii nzito nikaisikia vizuri kwenye masikio yangu, taa zote ndani ya chumba hichi zikazima na nikaona kivuli cha mtu chenye mwanga hafifu sana kikiwa kimesimama kwenye moja ya ukuta wa humu chumbani huku kivuli hicho kikionesha mtu huyo akiwa amevaa joho kubwa sana, ila haonekani kichwa ni kipi wala miguu ni ipi jambo lilo nifanya niaguke chini mzima mzima huku nikitamani kupiga kelele ila sauti yangu haikuweza kutoka.



“Usiogope, mimi sio mbaya kwako”

Sauti ya mwanaume huyu ikazidi kuniongelesha, jasho lililo tokana na joto kali likazidi kuniandama.

“Najua nini unacho kiwaza na kukifikiria. Nitakusaidia, kadri siku zitakavyo zidi kwenda ndivyo kadri nitakavyo zidi kuwa rafiki yako na msaada wako kwako. Usimuambie mtu wa aina yoyote habari hii umenielewa?”

Nikamjibu kwa kutingisha kichwa nikimaanisha kwamba nimelewa.

“Endapo utazungumza chochote kwa mtu yoyote basi mtu huyo nitamuua. Lala salama na usiku mwema”

Mara baada ya mwanaume huyo kuzungumza hivyo, taa zote zikawaka na kila kitu kikarudi kwenye hali yake, hapakuwa na pazia hata moja ambalo liliweza kutingishika. NIkasimama kwa haraka na kuanza kutembea hadi mlangoni ili nikawaeleze Bi Jane Klopp na mumewe habari hizi, ila nilipo kumbuka kwamba endapo nitamualeza yoyote atakufa, basi hamasa hiyo ya kuwaambia, ikaanza kutetea na mwishowe nikajikuta nikirudi kitandani mwangu na kuaa. Kusema kweli katika siku ambazo sikuwahi kulala ni hii ya leo, sauti ya mwanaume huyu ambaye sifahamu ni nani ikazendelea kujirudia kwenye masikio yangu.

Nikastuka baada ya kengele iliyo fungwa mlangoni humu kuanza kuita, nikatazama saa ya ukutani nikaona ni majira ya saa kumi na moja kasoro alfajiri. Nikakumbuaka kwamba jana usiku bibi Jane Klopp aliniahidi kwamba atakuja kuniamsha muda huu ili nianze kuajiandaa kwa ajili ya safari kwa maana ndege yetu inaondoka saa kumi na mbili asubuhi. Kengele ikaendelea kuminywa, taratibu nikashuka kiyandani na kuanza kutembea hadi mlangoni, nikaufunga mlango nakweli nikamkuta bibi Jane Klopp akiwa amejawa na tabasamu pana sana usoni mwake.

“Umeamkaje Ethan?”

“Salama mama, wewe je?”

Niliitikia huku nikijifanya kama nina usingizi mwingi, ila kwa namna moja ama nyingine sina usingizi wa aina yoyote zaidi ya woga wa tukioa ambalo nilikutano nalo jana usiku.

“Tumeamka salama, jiandae tuianze safari”

“Sawa mama”

“Haya”

Bi Jane Klopp akaondoka mlangoni kwangu, nikafunga mlango na moja kwa moja nikalifwata sehemu begi langu la nguo lilipo, nikafungua zipo ya pembeni, nikatoa mswaki wangu pamoja na dawa yake, kisha nikaelekea bafuni. Nikasafisha kinywa changu, ndani ya muda mfupi nikiwa tayari nimesha maliza kukisafisha kinywa hichi. Nikaoga haraka haraka kisha nikarudi chumbani, nikavaa nguo nilizo kusudia kuzivaa katika safari hii, ambayo tayari hamu yake imerudi kwenye mstari hata tukio lililo tokea jana usiku likaanza kunipotea kwenye upeo wangu wa akili.

Nilipo hakikisha kwamba nimemaliza kila kitu, nikamuomba Mungu kama nilivyo fundishwa na Bi Jane Klopp, ili awe kunitangulia katika safari hii, kisha nilipo maliza sala yangu, nikatoka chumbani humu huku nikilivuta begi langu. Kwa bahati nzuri nikakutana na Bi Jane Klopp pamoja na mzee Klopp wakitoka kwenye chumba chao huku nao wakiwa tayari wamesha jianda. Nikamsalimia mzee Klopp kwa heshima zote, kisha tukaelekea nje ya hoteli hii na kumkuta yule dereva ambaye alituleta jana hapa hotelini akiwa tayari amesha fika kama vile alivyo elezwa na bi Jane Klopp aweze kuwahi asubuhi na mapesa kwenye hotel hii.

Baada ya dereva kuingiza mabegi yetu nyuma ya taksi yake hii, mimi na bi Jane Klop tukaingia kwenye siti ya nyuma huku Mzee Klopp akipanda siti na kukaa siti ya mbele pamoja na dereva.

“Ethan mwanangu, unajisikiaje?”

Bi Jane Klopp aliniuliza huku akiwa amenishika mkono wangu wa kulia huku akiminya minya kiganja changu.

“Ndio mama, nina furaha sana”

“Unakwenda kuyaanza maisha mapya sasa Ethan”

“Kweli baba ninakwenda kuanza maisha mapya”

“Ila tutakuwa tunarudi Tanzania mara kadhaa, kuitembele hii nchi si unafahamu kwamba hii ndio nchi yako”

“Ndio mama”

“Hata ikatokea kwamba tumekufa, ila Tambua uhalisia wako wewe ni upi, wapi umetoka na tunaamini kwamba ipo siku utakuna na ndugu zako”

“Sawa mama”

Swala la ndugu zangu bado kwa upande wangu ni kitendawili, nina jaribu kuvuta kumbukumbu za kumkumbuka japo hata mama yangu wa kunizaa ila sipati hata taswira yake. Tukafika uwanja wa ndege, tukapitia hatua zote ambazo kama abiria anatakiwa kupitia, muda wa abiria kuelekea kwenye ndege tunayo paswa kusafiri nayo, ukawadia. Tukaingia kwenye ndege hiyo bibi Jane Klopp na mumewe wakaa katika siti za mbili huku mim nikikaa siti ya pembeni yao, ila na abiria mwengine ambaye ni mwana mama wa kiafrika. Nikamsalimia mwana mama huyu kwa heshima sana, hadi mwenyewe akanishangaa. Akaitikia salamu yangu huku akiwaametabasamu.

“Unaitwa nani mtoto?”

“Ethan Klopp”

“Anaa mimi naitwa mama Lukas”

“Nashukuru kukufahamu mama Lukas”

“Unasafiri peke yako?”

“Hapana, nipo na wazazi wangu, hao hapo”

Nikawaonyesha Bi Jane Klopp na mume, ambao nao kwa furaha wakasalimiana na mama huyu.

“Kusema kweli nimetokea kumpenda sana huyu mtoto ana heshima na maadili mazuri sana”

“Hata sisi tunampenda Ethan wetu kwani ni kijana mtiifu na mwenye hekima sana”

“Aisee muendelee kumkuza kwenye maadili haya haya. Hapa ninawaambia muna tunda lilo bora”

“Tunashukuru”

“Munaelekea wapi?”

“Sisi tunarudi Ujerumani, tulikuwa Tanzania, kwa kazi ya mwaka mmoja, imeisha wiki hii basi tunarudi kwetu, japo Mungu ametubariki tunarudi tukiwa na mtoto wetu”

“Hahaha kweli Mungu amewabariki kwa kweli, yaani nina watoto kama huyu. Ila niwakorofi hakuna, ila nilipo muona huyu na jinsi alivyo nisalimia, hakika nikaona kwamba ndani ya huyu mtoto kuna tunda lililo jema”

“Shukrani sana”

Bibi Jane alijibu huku akiwa amejawa na furaha sana kwani nyota yangu ya kupendwa na watu inaanza kukua sasa.

“Wewe Ujerumani unakwenda matembezi au?”

“No, ninakwenda kikazi, raisi ameniteua kuwa balozi kule jana mchana, na leo nimegizwa nikawasili ubalozini haraka iwezekanavyo baada ya hapo, basi nitafanya hatua za kuwahamishia watoto wangu nchini humo”

“Ohoo hongera sana”

“Asante sana, nilikuwa ni mkurugenzi wa shirika la Afya, ila raisi alivyo ona anapendezwa na utendaji wangu wa kazi basi ameniteua katika nafasi hiyo”

“Kweli weli, vipi lakini una watoto wangapi?”

“Watu, wa kike wawili ni mapacha, Jane na Judy, hao wana miaka kumi na mbili sasa na Lukas cha ukorofi ana miaka sita”

“Waoo, naona hapo nina wajina wangu”

“Hee…unaitwa Judy na wewe?”

“No ninaitwa Jane Klopp”

“Okay safi sana, ninashukuru kwamba nimepata wenyeji wangu na hongera una fahamu Kiswahili vizuri sana”

“Yaa ni kweli, nilijifunza kwa juhudi mimi na mume wangu basi tumeweza kukifahamu. Na hata Ethan naye amesha kifahamu Kijerumani”

“Aisee Ethan inabidi unifundishe na mimi Kijerumani”

Nikamsalimia Mama Lukas kwa lugha ya kijerumani, akabaki akinitazama tu na kushindwa kunijibu.

“Ndio umesemaje?”

“Nimekusalimia habari yako mama”

Mama Lukas akacheka sana kwani nilimuacha njia panda.

“Haki ya Mungu nimefurahi sana. Ninawaomba siku nikihamishia familia yangu huku, ninawaomba basi mtoto wenu awe na urafiki na Lukas wangu”

“Usijali hilo hadi sasa hivi tumesha kuwa marafiki, Mungu atatutangulia kwenye maisha ya huko mbeleni”

“Kweli kweli”

Sauti ya muhudumu akituomba tuweze kufunga mikanda ya siti tulizo kalia, ikakatisha mazungumzo ya bi Jane Klopp na mama Lukas. Mama Lukas, alipo ona nina hangaika kuufunga mkanda wa siti yangu akanisaidia, na akaubana vizuri kiunoni mwangu.

Huku nikiwa ninachungulia dirishani, nikaanza kuona jinsi ndege inavyo tembea kwani baadhi ya ndege zilizo simama, tunaziacha zilipo simama.

“Huogopi kuangalia nje?”

Mama Lukas aliniambia huku akinitazama.

“Hahaa hapana siogopi”

“Kweli?”

“Ndio”

Ndege ikaanza kunyanyuka taratibu, matumaini ya kuishi maisha mapya yakazidi kujengeka. Machozi yakaanza kunilenga lenga, kwani ninaiacha nchi ambayo ndio niliyo zaliwa. Ila kutokana na maisha tu ina bidi niondoke nchini hapa, huku moyoni mwangu nikiendelea kujiapiza kwamba ni lazima siku moja nihakikishe kwamba nimeiutawala mji wa Dar es Salaam, japo sifahamu nitautawala vipi. Uchovu wa kuto kulala usiku kucha ukanitawala, taratibu nikaanza kusinzia na mwishowe usingizi mzito ukanipitia..

“Ethan….amka upate chakula”

Sauti ya Mama Lukas, ikasikika vizuri masikioni mwangu, nikayafumbua macho yangu na kumtazma, nikamuona muhudumu wa kike akiwa amesimama pembeni yetu akijawa na tabasamu. Nikajiweka vizuri kwenye siti yangu huku nikijaribu kumtazama bibi Jane Klopp na mumewe sehemu walipo kaa wapo, bi Jane Klopp akanipungia mkono huku akiw ameshika sambusha mkononi mwake. Nikatabasamu kidogo kisha nikamtazama muhudumu.

“Unahitaji nini mtoto”

“Sambuza na juisi?”

“Ngapi?”

Nikamjibu kwa kumuonyeshea vidole vyangu vya mkono wa kulia, nikimaanisha kwamba ninahitaji sambusa tatu.

Muhudumu akaondoka na kutiacha na mama Lukas, ambaye naye anapata chakula aina ya tambi taratibu.

“Tumetembea sana enee?”

“Hahaa ndio hasi sasa tuna masaa manne angani”

“Sawa”

Muhudumu akaniletea nilicho muagiza, akanisaidia kunikunjulia kijimeza changu kilichopo pembeni ya siti yangu. Akaniweka chakula changu, akanikaribisha na kuondoka. Taratibu nikaanza kula sambusa moja huku nikiwa na furaha moyoni mwangu.

“Ethan”

“Naam”

“Unapenda kuwa nani mkubwani?”

Nikamtazama Mama Lukas kwa muda huku nikifikiria cha kumjibu, kwani maisha yangu ninahitaji kuwa mtu mwenye nguvu ila sifahamu ni nguvu ya namna gani ambayo ninatakiwa kuwa nayo.

“Aha…nahitaji kuwa mtu mzuri nitakaye pendwa na watu”

“Mbona hata sasa hivi ni mtu mzuri na unapendwa na watu. Maana ya swali langu ni kwamba unapenda kuwa nani, labda rubani kama hawa wanao endesha hii ndege, au mwalimu….”

“Ahaaa….ninataka kuwa mwana michezo”

“Mchezo gani unapenda?”

“Mpira”

“Kweli?”

“Ndio”

“Basi inabidi ujitahidi na kuwa kama kina Mbwana Samatta, je una mfahamu?”

Nikatingisha kichwa nikimaanisha kwamba simfahamu, mama Lukas akafungua pochi yake na kutoa simu. Akaanza kunionyesha picha za mchezaji huyo aliye nitajia jina.

“Huyu ni kijana Mtanzania, kwa sasa anacheza huko nchi za nje. Sasa na wewe kama unataka kuwa mchezaji wa mpira basi unatakiwa kujitahidi kuwa zaidi ya huyu”

“Ila yeye ni mkubwa tayari?”

“Yaa na wewe si utakuwa mkubwa, ukiwa tu mkubwa hakikisha kwamba unacheza mpira vizuri na uwe mahiri sawa”

“Sawa nitakua”

“Tupige”

Mama Lukas alizungumza huku akinionyesha kidole chake cha mwisho cha mkono wake wa kulia, tukakutanisha vidole vyetu na kumfanya bibi Jane Klopp na mume wake kutabasamu kwa kitendo hichi ambacho ni cha furaha sana.

“Yeah usipo kuwa tu mchezaji mzuri basi siku tukionana nitakuuliza kwa nini hujawa”

“Sawa”

Safari hii kusema kweli ni nzuri sana, sikujisikia unyonge hata kidogo kwenye ndege. Safari ya kutoka nchini Tanzania hadi Ujerumani, ikachukua msaa mia moja ha hamsini ambayo ni sawa na siku mbili na masaa saba. Tukafika nchini Ujerumani, ikiwa ni majira ya usiku. Baridi kali ya nchi hii, ni tofauti kabisa na baridi ya nchini Tanzania tena kule Arusha nilipo kuwa nikiishi. Tukaagana na mama Lukas, akaingia kwenye gari alilo kuja kuchukuliwa watu wa Ubalozini kisha nasi tukapanda gari nzuri sana ya milango sita ambayo mzee Klopp na mkewa wamekuja kuchukuliwa.

“Hapa ni Berlin ukiwa unasoma kwenye masomo ya historia, utaweza kusoma mji hu wa Berlin. Hapa ndipo ulipo fanyika mkutano wa kusuluhisha vita kuu ya dunia”

Mzee Klopp aliniambia huku akinionyesha majengo makubwa na mazuri kuliko hata yale niliyo yaona jijini Dar es Salaam.

“Ni pazuri?”

“Yaaa hapa ni pazuri sana, ila kesho mama yako akipata muda basi unaweza kukutembeza na ukazidi kufahamu uzuri wa eneo hilo”

“Usihofu Ethan, tutatembea karibia nchi nzima ili mradi tu uweze kuifahamu vizuri sana, kwa maana muda wa kuanza shule bado”

“Yaa utaanza mwezi ujao”

“Sawa sawa wazazi wangu”

“Sisi hapa Berlin tuna makampuni yetu mawili, moja inahusika na maswala ya kutengeneza magari na nyengine ni hospitali inayo husika na magonjwa ya moyo”

“Ahaaa”

“Katika hiyo hospitali, dada yako ndipo anapo fanyia kazi, yeye ndio msimamizi mkuu wa hospitali hiyo”

Bibi Jane Klopp alinipa maelezo hayo niliyo yaelewa vizuri sana. Tukafika katika jumba moja kubwa sana lililo zungukwa na miti mingi na mirefu sana kwenda juu.

“Hapa ndipo tunapo ishi, kidogo tupo nje ya mji. Tumesha kuwa wazee sasa na hatuwezi kukaa mjini”

“Ahaa”

Taratibu geti likafunguka na gari likaanza kuingia taratibu hadi kwenye eneo la kusimamia. Nikamuona binti mmoja mrefu akiwa amesimama nje huku akionekana kujawa na shahuku kubwa sana ya kuweza kuwaona watu walipo ndani ya gari. Taratibu dereva akatufungulia mlango, akaanza kushuka mzee Klopp, binti huyo akamkumbatia baba yake kwa furaha sana, akashuka bibi Jane Klopp kisha nikafwatia mimia. Binti huyu akamkumbatia bibi Klopp.

“Mery kutana na Ethan”

“Mambo Ethan”

Binti huyu alizungumza kwa furaha kidogo.

“Safi tu dada”

Ethan huyu ni Mery ndio yule binti yetu tuliye kuambia.

“Nashukuru kukutana na wewe dada Mery”

Nilizungumza huku nikimpa Mery mkono, akautazama kwa muda mkono wangu kisha akaupotezea na kujifanya ana kwenda kusaidia kushusha mabegi kwenye gari. Kitend hichi kusema kweli kikanifanya nijisikie vibaya hadi Mzee Klopp na mkewa walakifahamu hilo.

“Mzoe si unajua madaktari wana mambo mengi”

Bi Jane Klopp alijitahidi kunifariji, ila hata wao hawakupendezewa na jambo hili. Tukangia ndani ya jumba hili kubwa, kusema kweli ni jumba ambalo limejengeka vizuri sana. Bibi Jane akanionyesha chumba changu cha kulala, nikaweka begi langu kisha tukarudi sebleni na kupata chakula kilicho andaliwa vizuri sana. Ila muda wote nikajikuta nikimtazama Mery na kujiuliza ni kwa nini amenidharau.

“Mery unatakiwa kumuomba msamaha Ethan kwa kuto kuupokea mkono wake.”

Mzee Klopp alizungumza huku akinimtazama Mery.

“Baba na mama pasipo kuwavunjia heshima siwezi kumuomba huyo sokwe msahama, na inakuwaje munaleta Masokwe nyumbani kwetu na wala hamjanishirikisha eheee?”

Kauli hii, ikaulipua moyo wangu, hasira ikapanda na kunifanya mwili mzima kunitetemeka, glasi ya juisi niliyo ishika mkoni mwangu, nikajikuta ikiniponyoka na kuanguka chini jambo lililo wafanya watu wote kunishangaa.



Nikanyanyuka kwa hasira kwenye kiti changu na kukimbilia chumbani kwangu huku machozi yakinimwagika usoni mwangu. Nikajitupa kitandani na kuendelea kulia, hazikupita hata dakika mbili bi Jane Klopp akaingia chumbani humu, taratibu akaka kitandani na kunikumbatia na kuanza kunibembeleza huku akioniomba niweze kuwa mvumilivu na mtoto wao atanielewa tu.

“Kwa hiyo mimi ni Sokwe?”

Nilizungumza kwa sauti ya chini iliyo jaa upole na masikitiko mengi sana, japo ni mtoto ila swala la kudharauliwa na kuitwa sokwe kusema kweli limeniumiza sana moyo wangu.

“Hapana Ethan, watu wote sisi ni sawa mwanangu, wala usijisikie vibaya”

Bibi Jane Klopp akatumia muda mwingi sana katika kunibembeleza hadi nikapitia wa usingizi. Ubaridi mkali ulioa ambatana na upepo ukanifanya niweze kuzinduka usingizini, nikatazama chumba kizima na kukuta mwanga hafifu wa mbala mwezi unao ingia kupitia dirisha ambalo lipo wazi. Taratibu nikashuka kitandani na kuanza kutembea kuelekea lilipo dirisha hilo ili niweze kulifungua. Kabla sijalifikia sauti ya mwanaume ambaye aliniita kipindi nilipo kuwa hotelini, ikaniita tena nyuma yangu. Nikastuka sana na kugeuka, nikaona kivuli kikiwa ukutani.

“Ethan pole sana kwa kile kilicho kukuta”

Sauti ya mwanaume huyu ilizungumza na kunifanya niingiwe na hofu.

“Usiogope, natambua kwamba umefedheheka sana moyoni mwako, ila nina kitu ninahitaji kukuonyesha”

“Kitu gani?”

“Twende nje”

“Nje, wapi?”

Niliuliza kwa kujikaza tu, ila kusema kweli nina wasiwasi mwingi.

“Wewe twende tu”

Nikahisi hali ya kujiamini moyoni mwangu, taratibu nikaanza kutembea kuelekea mlangoni.

“Hapana usipitie mlangoni”

Sauti ya mwanaume huyu iliendelea kunielekeza, na hali ya kuiogopa yote imenitoweka.

“Wapi nipitie?”

“Dirishani pale”

Nikatembea hadi dirishani na kuchungulia nje.

“Nitatokaje hapa wakati kuna gorofa?”

“Wewe ruka hadi chini?”

“Acha kunitania, nitarukaje hadi chini. Unataka nivunjike”

“Kumbuka kwamba nilisha kueleza nipo kwa ajili ya kukusaidia, kwa hiyo siwezi kukuacha uumie”

Nikajishauri kwa sekunde kadhaa, akili za utoto nahisi nazo zinachangia, kwani sikuhitahi kufikiria jambo hili kwa mapana na kujaribu kile ambacho nina ambiwa. Taratibu nikapanda dirishani na kujirusha kwenda chini huku nikiwa nimeyafumba macho yangu.

Kitu kilicho nishangaza ni kuto kufika chini ya ardhi, nikafumbua macho yangu kwa haraka sana. Nikajikuta nikiwa nina ambaa hewani huku chini ya ardhi kukiwa na ukungu mwingi sana kama tulio zoea kuuona Moshi majira ya asubuhi au usiku.

“Usiogope”

“Umefanya nini sasa mbona sikanyagi chini?”

Niliuliza huku mapigo ya moyo yakinienda mbio.

“Unaniamini?”

“Ehee…..!!?”

“Unaniamini kama rafiki yako?”

“Nitakuaminije ikiwa sikuoni sura yako”

“Unataka kuniona sura yangu?”

“Ndio”

“Twende”

Tartaibu nikaanza kuona nikiondoka katika eneo nililopo, nikatamani kujifinya ili mardi niweze kuona kama nipo ndotoni au laa, ila kila kinacho tokea ni jambo la ukweli na si ndoto kabisa. Tukazidi kupita juu yam situ huu uliopo karibu kabisa na msitu wa jumba la mzee Klopp na mkewe.

“Tunaelekea wapi?”

“Ninataka kukuonyesha Ujerumani jinsi ilivyo”

“Sasa utanionyeshaje ujerumani ilivyo ikiwa hutaki nikuone sura yako”

“Utaniona tu siku, muda bodo haujafika”

Nikaanza kuona majengo mengi makubwa kwa juu. Majengo haya yote yamejengwa kwa ustadi wa hali ya juu, akaanza kunielezea kila mji na sifa zake pamoja na asili ya watu wake. Kusema kweli ni jambo ambalo linanifurahisha moyoni mwangu na kuniburudisha.

“Kwa nini umekuwa rafiki yangu na unaitwa nani?”

“Hahaaa…..”

Sauti hii ya kiume ilicheka kidogo.

“Jina langu ni gumu sana, nitakutajia siku nyingine”

“Kwa nini?”

“Usijali nitakuambia, kuna mambo mengi sana nahitaji tufanye pamoja na yakikamilika basi nitakueleza na utanijua”

“Haya kwa nini umenipenda mimi?”

“Hahaa….niyauambia pia hiyo siku ikifika”

Tukaendelea kuzunguka hadi ilipo kuwa ikaribia majira ya asubuhi, akaniridisha hadi chumbani kwangu, kisha akaniaga na kuondoka jambo ambalo kusema kweli linazidi kunishangaza. Nikapanda kitandani taratibu huku nikiwa nimejawa na furaha kubwa sana ya kuiona miji ya nchi hii ya Ujerumani. Usingizi taratibu ukaanza kunipitia na nikalala fofofo.

Bibi Jane Klopp akaniamsha, akanieleza juu ya safari ya matembezi na kwenda kuiona shule ambayo ninatakiwa kuanza masomo yangu ya shule ya msingi.

“Jiandae”

“Sawa mama”

Nikaingia bafuni, nikajisafisha kinywa changu na kuoga, baada ya kumaliza, nikavaa moja ya suti ya kijivu ambayo bi Jane Klopp alininunulia. Nikatoka chumbani humu na kuelekea sebleni, nikakutana na Mery akiwa amevalia suti nyeusi, nikajaribu kumsalimia ila hakiniitikia zaidi ya kunipita.

“Dada Mery nimekusalimia”

“Wewe nguruwe mdogo nimekuomba salamu yako”

Mery alizungumza huku akinitazama usoni mwangu kwa hasira.

“Nikiwa kama mdogo wako ni lazima nikupatie heshima”

Nikastukia kofi usoni mwangu jambo lililo nifanya nijisikie vibaya sana.

“Mery ni nini unacho fanya?”

Mzee Klopp alizungumza kwa ukali huku akishuka kwenye ngazi.

“Nimewaambia huyu Sokwe, sijui nguruwe, sitaki kumuona huku”

“Hiyo sio tabia tuliyo kufundisha sisi wazazi wako lakini?”

Mzee Klopp alilalama kidogo.

“Kwa nini munanikosesha amani eheee, khaa”

Mery akatoka humu ndania kiwa na jazba, mzee Klopp akanifwata nilipo simama na kunikumbatia.

“Ethan, kila kitu kinakwenda kukaa vizuri sawa mwanangu”

“Sawa baba”

Nilijibu huku machozi yakinilenga lenga usoni mwangu. Nikaanza kuhisi magari yakigongana huku moja likipinduka vibaya sana. Katika ufahamu wangu wa akili nikamuona Mery akiwa ndani ya gari hilo lililo pinduka. Nikatamani kuzungumza hisia zangu ninazo zihisi ila nikashindwa kutokana na kuogopa, nikamuachia mzee Klopp na kuanza kukimbilia nje, kwa mbali nikaliona gari ambalo amepanda Mery likitoka kwenye geti na gari hilo ndio nililo liona kwenye hisia zangu na hii ndio mara yangu ya kwanza kuliona.

“Achana naye akirudi jioni tutazungumza naye”

“Baba”

“Naam”

“Nitakacho kuambia utaweza kukiamini?”

“Yaa kwa nini nisikuamini”

“Naomba umzuie dada Mery asiende anapo kwenda?”

“Kwa nini?”

“Ninahisi kuna ajali itatokea?”

“Ajali?”

“Ndio baba”

Mzee Klopp akaonekana kuelewa kile nilicho kizungumza. Akatoa simu yake mfukoni na kuanza kuminya minya, akaiweka sikioni kwa sekunde kadhaa ila akaishusha, akarudia tena kuiweka simu yake sikioni ila baada ya muda mchache tena akaishusha.

“Anakata simu”

Mzee Klopp alizungumza huku akiwa na wasiwasi mwingi sana. Bibi Jane Klopp akatoka ndani huku akiwa amependeza sana.

“Mbona muna wasiwasi kuna nini kinacho endelea?”

“Ethan muambie mama yako”

Mzee Klopp alizungumza huku akiendelea kumimnya minya simu yake na kuiweka sikioni.

“Eti Ethan ni nini kinacho endelea?”

“Ninahisi kuna ajali mbaya itampata dada Mery”

Bibi Jane Klopp wasiwasi mwingi ukamjaa.

“Mume wangu tutafanya nini?”

“Najaribu kumpigia anakata simu, amempiga mtoto wa watu hapa anahisi labda ndio hilo jambo ninataka kuzungumza naye”

“Mpigie dereva wake”

Mzee Klopp akafwata ushauri wa mke wake.

“Ehee upo wapi?”

“Nyumbani…..unafanyaje?”

“Ohooo Mungu wangu haya”

Mzee Klopp akakata simu huku akionekana kuwa na wasiwasi mwingi.

“Alimuambia dereva wake asije leo kazini”

“Mungu wangu, ngoja nijaribu kumpigia mimi”

Bi Jane Klopp akatoa simu yake kwenye pochi, akapiga namba ya Mery, sura yake jinsi ilivyo anza kubadilika dhairi ikaonyesha kwamba kuna tatizo limejitokeza.

“Kuna nini mke wangu”

“Nimesikia kishindo kizito na siu ikakata”

“Ohooo…Mungu baba ni nini tena kimempata”

Bibi Jane Klopp akaanguka chini, jambo lililo tufanya tuchanganyikiwe. Wafanyakazi kwa haraka wakafika katika eneo hili na kusaidiana na mzee Klopp kumuingiza ndani bi Jane Klopp. Simu ya mzee Klopp ikaanza kuita, akaitazama kwa muda huku akinitazama usoni mwangu. Akaipokea simu yake na kuiweka sikioni.

“Ndio ni mimi”

Nikamuona Mzee Klopp machozi yakimlenga lenga. Taratibu akaka kwenye kochi akionekana dhairi kwamba amechoka kwa taarifa alizo pewa.

“Sawa ninakuja”

Mzee Klopp alizungumza kwa uonge huku akinitazama usoni mwangu. Taratibu akanyanyuka na kunishika mkono na tukaanza kupandisha kuelekea gorofani.

“Ethan umejuaje kama mwanangu atapata ajali?”

“Eheee?”

“Ulijuaje?”

Mzee Klopp alizungumza kwa ukali kidogo.

“M…imi…nimehisi tu”

“Unahisi umekuwa malaika wewe?”

Mzee Ethan alizidi kufoka hadi sura ikaanza kuwa nyekundu jambo lililo nifanya nianze kupata woga.

“Na akifa mwanangu utanitambua”

“Likini bab…..”

“Koma mimi sio baba yako, mwanangu ni mmoja na anakimbizwa hospitalini sasa hivi unaniambia nini nikuelewe mjinga weweee”

Maneno ya mzee Klopp yakanikatisha tamaa kwa kweli ya kuendelea kuishi humu kwenye nyumba yake, kwa kweli kwa hapo awali nilihisi kwamba nitayafurahia maisha yangu ya hapa nchini Ujerumani, ila kile nilicho kifikiria sicho kinacho nitokea na nimekuwa ni tatizo toka niingie jana kwenye hili jumba.



Mzee Klopp akatoka ndani humu na kuniacha nikiwa nimejawa na woga ulio ambatana na wasiwa mwingi sana.

“Utanata na huyu tumfanye nini?”

Sauti ya mwaume ambayo ninaihisi mimi mwenyewe ilizungumza na kunifanya nistuke kidogo.

“Ethan, unataka tumfanyaje na huyu mzee”

“Ngoja kwanza, unataka kuniambia kwamba wewe ndio msababishaji wa tatizo hili?”

“Ndio”

“Kwa nini sasa umesababisha”

“Kila ambaye anakujeruhi moyo wako, nilazima nihakikishe kwamba analipa kwa garama ya damu yake kumwagika”

“Ila umesikia nilichoa ambiwa hapa, kama dada wa watu akifa itanigarimu”

“Hawezi kufa”

“Kama hawezi kufa naomba unisaidie basi apone”

“Usijali, atapona”

“Sasa nitafanyaje?”

“Nenda sebleni, ukajumuike na bibi Jane, mutakwenda hospitali moja”

“Sawa”

Nikatoka ndani humu na kurudi sebleni, nikawakuta madaktari wakiwa wanampakiza bibi Jane Klopp kwenye machelea. Tukatoka ndani humu na wakamuingiza kwenye gari la wangonjwa na mimi nikaingia ndani ya gari hili na tukaondoka katika eneo hili.

‘Ehee nimekuja nipo na wewe, usizungumze kwa sauti, wewe niulize hata ndani ya nafsi yako ninaweza kukusikia na kukujibu’

Niliisikia sauti ya mwanaume huyu ikiendelea kuwa nami, jambo lililo nifanya nistuke kidogo ila manesi hawakuwea kugundua jambo lolote

‘Sasa kwa nini bibi Jane ameanguka’

‘Amestuka tu, ila atakuwa poa muda si mrefu’

‘Fanya azinduke sasa hivi bwana’

‘Ngoja tufike hospitalini’

‘Hapa huwezi ukamfanya akazinduka?’

‘Ninaweza, mshike mkono wake wa kulia’

Taratibu nikamshika bibi Jane Klopp mkono wake wa kulia, hazikupita hata sekunde tano bibi Jane Klopp akafumbua macho yake hadi manesi wakastuka kidogo.

“Ethan”

“Ndio mama”

Bibi Jane Klopp akawatazama manesi hawa.

“Mery yupo wapi?”

“Baba ametangulia hospitalini kumtazama”

“Amelazwa hospitali gani?”

Nikashindwa kulijibu swali hili kwa maana sifahamu ni hospitali gani.

‘Ni hospitali gani?’

‘Sio jukumu lako kumjibu subiri mutafika’

Baada ya muda tukafika hospitalini, bibi Jane Klopp akashuka huku akiwa kwenye kitanda hichi cha wagonjwa. Akapelekwa kwenye chumba cha mapumziko kwa muda huku nikijumuika naye. Baada ya muda kidogo akaja daktari aliye weza kutueleza juu ya eneo alipo Mery.

“Ethan hii ni hospitali yetu”

Bibi Jane Klopp alizugumza huku tukiwa tumeongozana na daktari huyu.

“Ahaa…hii ndio inayo simamiwa na dada Mery?”

“Ndio”

Tukafika nje ya mlango wa chumba cha upasuaji, tukamkuta mzee Klopp akiwa anazunguka zunguka tu. Akakumbatiana na mkewe, ila mimi hakushuhulika nami.

‘Usijali atakuwa salama’

Niliisikia sautu ya rafiki yangu huyu.

‘Una uhakika?’

‘Ndio’

Tukaendelea kusubiria zaidi ya masaa mawili. Mery akatolewa kwenye chumba cha upasuaji na kupelekwa kwenye chumba cha wagonjwa mahututi ambacho kimeandikwa kwa lugha ya kijerumani intensivmedizin.

“Ahaa wewe usiingie”

Mzee Klopp alizungumza huku akinizuia kuingia katika chumba hichi, jambo lililo mshangaza sana bi Jane Klopp. Sikutaka kuwa mbishi zaidi ya kukaa nje ya chumba hichi nikisubiria watoke katika chumba hicho. Baada ya muda kidogo wakatoka wakiwa wamejawa na sura za tabasamu kidogo.

“Anaendeleaje dada?”

“Yupo vizuri kiasi, madaktari wamesema kwamba watamlaza kwa siku chache kisha watamruhusu kurudi nyumbani?”

Bi Jane Klopp alinijibu kwa upole na unyenyekevu sana.

“Ameumia vibaya?”

“Hapana ni majeraha macheche, ila mguu wa kushoto ulivunjika mara mbili”

Mzee Klopp alinijibu kwa upole hadi mimi mwenyewe nikashangaa.

Siku zikazidi kusonga mbele huku hali ya Mery ikazidi kuimarika. Urafiki wangu na huyu rafiki yangu nisiye muona ambaye kwa haraka haraka ninaamini kwamba ni jini, zikazidi kusonga mbele. Siku ya kuanza masomo yangu rasmi kwenye shule ya msingi ya Berlin Metropolitan.

Nikaongozana na Bi Jane Klopp hadi kwenye shule hii na kutokana na umaarufu wa bibi huyu, waalimu waliweza kunifahamu kwa haraka sana.

“Ujitahidi mwanangu”

“Sawa bibi nitajitahidi”

“Kitu kingine hakikisha kwamba unakuwa na upendo na wezako, heshima na ukarimu kwa kia mtu. Pia jifunze kuwa na utamaduni wa kuwasaidia wezako pale anapo shindwa kwenye masomo”

“Sawa sawa mama”

“Nitakuwa ninakuja kukutembelea kila mwisho wa wiki ili kufahamu una endeleaje”

“Sawa mama”

Tukaagana na bi Jane Klopp, kisha nikabaki chini ya uangalizi wa mwalimu aliye weza kujitambulisha kwamba ni mwalimu wa michezo. Nikapelekwa bwenini, na kuingizwa kwenye chumba chenye viyanda viwili vya juu na chini.

“Kuna mwenzako mmoja amefika leo amachagua kitanda hichi, wewe utapenda kulala kitanda cha juu au chini?”

“Hichi hapa”

Nilichagua kitanda cha juu, kisha nikachagua kabati langu la kuhifadhia nguo na vitabu. Katika siku mbili hizi, waalimu na walezi wa wanafunzi walikuwa bize katika kuwapokea wanafunzi wa darasa la kwanza kutoka maeneo mbali mbali ndani na nje ya nchi ya Ujerumani, katika wanafunzi wenye asili kutoka barani Afrika, hatuzidi kumi huku mimi ndio nikiwa Mtanzania pekee. Kitu nilicho weza kukigundua kwa haraka haraka kwa baadhi ya wanafunzi, ni wabaguzi wa rangi. Sisi wanafunzi weusi tunaonekana kama watu wa ajabu sana ambao hatuna thamani na uwezo wowote mbele yao.

‘Kwa nini wanatunyanyasa?’

Nimuuliza rafiki yangu huyu siku nikiwa nimekaa mwenyewe kwenye moja ya benchi la mapumziko, ambalo wanafunzi wengine wenye asili ya kizungu waliliacha kisa nimekaa mimi, kwa bahati mbaya sina rafiki zaidi ya yule ninaye lala naye chumba kimoja na yeye urafiki wetu ni usiku tu pale tunapo kuwa tumerudi kulala bwenini.

‘Unatakiwa kuhakikisha kwamba una wazidi kwa kila kitu’

‘Kwa kila kitu kivipi?’

‘Darasani hadi kwenye michezo’

‘Mmmm sasa masomo yenyewe ni magumu na wezangu wenyewe wana jibu maswali kuliko hata mimi’

‘Usijali huu ni mwanzo tu ila utafahamu kila kitu kinavyo kwenda’

Nikastuka baada ya kuguswa mgogoni, nikageuka nyuma nikakutana na kundi la watotoo wezangu kama sita hivi huku aliye nigusa ni kibonge na mrefu kwenda juu.

“Wewe mtu mweusi toka kwenye hili benchi”

Alizungumza kwa lugha ya Kijerumani huku akinitazama kwa sura inayo onyesha ana maanisha kwa kile anacho kizungumza.

“Hutusikii”

Kibonge alizungumza huku akinishika shati langu la shule, nikajaribu kukataa, ila kwa nguvu zake alizo nazo akanivuta kwa nguvu na kuniangusha chini. Wanafunzi wote katika hili eneo wakabaki wakishangaa tukio hili, machozi yakaanza kunilenga lenga, kwani Kibonge na wezake wote wananicheka huku wanafunzi wengine wasio na huruma nao wakinicheka.

“Watu weusi nyinyi ni masokwe tu”

Kibonge alizugumza huku akitoa ndizi kwenye mfuko wa suruali yake. Akaimenya kisha akanipiga na ganda la ndizi hiyo usoni mwangu, jambo lililo zidi kuongeza vicheko kwa watu wengi. Nikiwa katika hali ya simnzi na kujisikia vibaya, akasimama dada mmoja mdogo mdogo kama sisi mbele yangua, akanitazama kwa sura ya huruma kisha akanipa kitama cheupe kwa ajili ya kujifuta machozi. Kibonge akampokonya mtoto huyu wa kike kitambaa hichi kabla ya hata sijakipokea.

“Mrudishie kitambaa chake”

Mtoto huyu wa kike mwenye asili ya Kijerumani alizungumza kwa ukali kidogo na kuwafanya bonge na wezake kucheka cheka. Mtoto huyu wa kike akamzaba bonge kofi zito la shavuni na kuwafanya wezake kuguna. Bonge akanyanyuka kwa hasira kwenye kiti alicho kikalia, akataka kumpiga mtoto huyu, ila jamaa wawili walio valia suti nyeusi na miwani yeusi wakafika katika eneo hili na kumkinga mtoto huyu.

“Mrudishie kitambaa”

Jamaa mmoja alizungumza kwa ukali kidogo, taratibu bonge akarudisha kwa msichana huyu, kisha akanipatia mimia.

“Pole mwaya”

“Asante”

“Unaitwa nani?”

“Ethan Klopp”

“Ohoo ni jina zuri, baadae”

Msichana huyu baada ya kuzungumza hivyo akaondoka na walinzi wake hawa wawili jambo lililo nishangaza sana, kwa maana wanafunzi wote hatuna walinzi, inakuwaje yeye awe na walinzi. Kutokana sina sehemu yak ukaa, nikaamua kurudi zangu darasani ili kumalizia kipindi cha mwisho kabla ya kuruhusiwa kwenda kula kisha baada ya bapo tutaendelea na mambo mengine.

‘Mbona umeniacha nidhalilike kwa kina Bonge?’

Nilimuliza rafiki yangu kwa maana yeye ndio niliye mzoea kuzungumza naye mambo mengi sana’

‘Ulitaka nikufanye shujaa wa kupigana au?’

‘Ndio’

‘Umesahau uliyo ambiwa na mama yako juu ya kuishi na watu vizuri?’

Kabla sijamjibu, wanafunzi wengine wakaingia darasani, akiwemo bonge na kundi lake. Wakanitazama kwa muda huku wakionekana kuchukizwa nami. Mwalimu akaingia na kuanza kutufundisha somo la historia. Kwa mara ya kwanza na mimi leo nikaulizwa swali na mwalimu na nikalijibu kwa ufasaha. Wanafunzi wezangu wakaombwa na mwalimu wanipigie makofi, ila wakanipigia wachache na wengine wakaa kimya. Sikuona hatua yoyote ambayo mwalimu aliichukua kwa wale ambao hawajanipigia makofi, nikajua kwamba ubaguzi wa rangi haupo kwa wanafunzi wezangu tu kumbe hata kwa waalimu.

Somu hili likaisha na tukatoka darasani na kuelekea kwenye holi kubwa la kupatia chakula. Kama kawaida, nikapanga foleni ya kwenda kuchukua chakula. Bonge na wezake wakafika na wakakaa mbele yangu kinguvu.

“Mumenikuta lakini”

Niliwaambia kwa lugha ya Kijerumani. Bonge akanigeukia, kitendo cha kunitazamana tu, nikajikuta nikiwa nipo kimya kutokana na kumuogopa. Nikasubiria bonge na wezake wachukua chakula kisha ikafwata zamu yangu ya kuchukua.

“Leo lazima utakoma”

Bonge alizungumza huku akinipiga kikumbo kidogo, bado nusu niagushe chakula changu ambacho ni wali na kuku. Nikaangaza angaza kwenye kila meza, nikaoga meza moja ikiwa ina jamaa mmoja mkubwa kidogo, taratibu nikaisogelea kisha nikaka kwenye kiti, jamaa huyu akanitazama kwa mcho makali, hadi nikatamani kuhamia katika meza nyingine.

“Dogo hujaona wa kukaa nao?”

“Ehee?”

“Hujaona wa kukaa nao?”

Taratibu nikanyanyuka na sahani yangu, nikaangaza maeneo mengine, nikaona meza moja wakinyanyuka kundi la wavulana wakubwa, nikafika katika meza hiyo waliyo ichafua kwa kumwaga mwaga chakula, kisha nikaa na kuanza kula.

‘Nachukia haya maisha ni bora niache shule tu’

Nilizungumza kimoyo moyo huku machozi yakinilenga lenga usoni mwangu.

‘Kwa nini?’

‘Nitaishije hivi kwa kunyanyaswa siku zote?’

‘Wata kuheshimu siku moja, piga moyo konde na pambana’

‘Nipambane vipi sasa, ikiwa kila mmoja ananichukia’

‘Si kwa yule aliye kupatia kitambaa chake’

‘Yule kwani ni nani?’

‘Ni mjukuu wa kwanza wa raisi wa hii nchi’

‘Kwa hiyo ni mjukuu wa raisi’

‘Ndio’

‘Sasa kwa nini amesoma shule hii?’

‘Hivi unahisi kwamba shule hii ni ndogo, hadi wewe kusoma hapa tambua kwamba una bahati kubwa sana, na acha kujidharau, chukulia haya maisha ambayo unaishi hapa ni ya kawaida, pambana katika masomo’

‘Mbona umekuwa ni mtu wa kunishauri tu, ila hunisaidi kwenye shida’

‘Ethan kumbuka kwamba mimi sio mtu’

‘Ni nani sasa, ikiwa tunazungumza na wewe unanisikia’

‘Muda na wakati ukifika basi utanifahamu, baade nina mambo ya kushuhulikia’

‘Wewe…..wewe…..’

Nilijitahidi kumuita ila hakuitika. Nikamaliza kula na nikaacha chombo changu hapa hapa juu ya meza kama utaratibu wa kawaida, kwani kuna wafanyakazia maalumu hushuhulika katika swala la kuosha vyombo, nikarudi bwenini, nikavua nguo zangu, nikajifunga taulo na kueleka katika bafu ambalo tunatumia wanafunzi wa darasa la kwanza kwenye bweni hili. Nikavua taulo langu na kulitundika kwenye msumari, nikajifunga taulo langu kisha taratibu nikaanza kuoga, nikiwa nimejipaka mapovu mwili mzima, akaingia bonge na kundi lake na wakaanza kunicheka huku wakizunguka jambo lililo sababisha nijawe na woga mwingi sana.



“Wewe sokwe unajifanya hodari kupendwa na wasichana wetu si ndio?”

Bonge alizungumza huku akinisukuma sukuma, kwa woga nilio nao nikajikuta nikishindwa kufanya jambo lolote zaidi ya kushika sabuni yangu walio nikuta nayo.

“Mshikeni”

Bonge aliwaamuru wezake, ambao kwa haraka wakanishika mikono yangu, jambo lililo nifanya nianze kulia hata kabla sijapigwa.

“Hehehee, linalia jinga hili”

Bonge alizungumza hukua kicheka na kuwafanya wezake wote walio nishika kuanza kucheka kwa dharau, bonge akaanza kunipiga vibao vya mashavuni huku akiendelea kunicheke. Nikajitahidi kwa nguvu zangu ili mrdi nijitetea kwa vijana hawa ila sikuweza kufanya chochote zaidi ya kuendelea kupigwa vibao vya unyanyasaji na bonge huyu. Akanipokonya sabuni yangu na kuanza kunipakaza nayo kichwani kwa nguvu hadi nikaanza kunishi maumivu.

“Nataka hii rangi yako nyeusi itokea mwilini mwako”

Bonge alizungumza huku akiendelea kunisugua sabuni hii mwilini mwangu huku akihamia mgongoni mwangu. Kusema kweli machozi ya hasiri yalizidi kunimwagika. Baaada ya bonge kunifanyia vitendo hivi vya unyanyasaji, akaniamshirisha wezake kuniachia na nikaanguka chini huku nikilia kwa uchungu sana. Wakaongeza nguvu ya bomba hili la maji kisha wakatoka bafuni humu huku wakicheka sana. Taratibu nikanyanyuka huku moyoni mwangu nikijiapiaza kulipiza kisasi kwa bonge na wezake. Nikajitahidi kuoga huku nikiendelea kububujikwa na mchozi, nikamaliza na kurudi chumbani kwangu. Nikabadilisha nguo na kuvaa nguo za michezo huku nikiendelea kuwa na hasira yangu. Nikachukua viatu vyangu vya kuchezea mpira na kueleka uwanjani. Nikawakuta wanafunzi wa darasa la kwanza wakipangwa nani aanze kucheza kwenye mechi ya darasa la pili. Bonge na wezake nao ni miongoni mwa wachezaji walio jitolea katika kucheza mechi hii.

“Ethan”

Mwalimu wa michezo wa darasa langu aliniita huku akinitazama.

“Naam”

“Mbona macho yako ni mekundu, vipi una umwa?”

“Hapana mwalimu”

Nilijibu huku nikitazama chni, mwalimu kwa ishara akaniita na kuniwekea kiganja cha mkono wake wa kulia shingoni mwangu ili kunipima joto la mwilini mwangu.

“Joto lako lipo vizuri”

Aliniambia huku akiendelea kunishika shika kwenye shingo yangu.

“Ben”

Mwalimu na Bonge akaitika, hapa ndipo nikafahamu jina halisi la bonge.

“Unacheza namba gani?”

“Mfungaji mwalimu”

Nikatamani kucheka kwa kweli, kwa maana huyo anaye sema anaweza kucheza nafasi ya ufungaji ni kibonge hata kutembea kwake ni shuhuli, kinacho mpa uhodari kidogo ni wezake anao tembea nao. Mwalimu wa darasa letu akapanga kikosi chake cha kwanza na mimi na wezangu wengine tukabaki nje. Wachezaji wakapewa jeshi na wakaingia kiwanjani.

“Mbona wewe hujachaguliwa?”

Sauti ya kike ikanistua na kugeuka nyuma, nikamuona binti aliye nisaidia muda wa machana nilipo kuwa nina nyanyaswa na kina bonge akiwa amesimama nyuma yangu huku na yeye akiwa amevalia nguo za mazoezi na walinzi wake wakiwa pembeni yake.

“Nitacheza tu”

“Nawewe kukaa”

Aliniuliza huku akionyesha sehemu ya pembeni yangu ambayo haina mtu katika benchi hili.

“Sawa unaweza kukaa”

Taratibu akakaa huku akiwa na tabasamu pana sana.

“Kwa nini wewe hujaenda kucheza na wezako”

“Mimi sipendelei sana michezo ya kike, ninapenda sana mpira”

“Mmmm….sasa huku wanacheza wanafunzi tu wa kiume?”

“Yaa ila nikipata nafasi na mimi nitacheza”

“Hahaaa..unapenda kucheza nafasi gani?”

“Golikipa”

“Weeee huoni ni nafasi ambayo ni hatari”

Msicha huyu hakunijibu chochote zaidi ya macho yetu kuyapeleka golini kwetu na tukashuhudia goli likiingia kwneye nyavu ya goli letu. Mpira ukaanza tena, mwanafunzi mwenzetu akampatia pasi bonge, ila bonge badala ya kupiga pira akapiga hewa na kuanguka chini kama kifurushi cha chumvi. Nikamuona mwalimu akifumba macho yake kwani yeye ndio kama kocha.

“Hhahaa ujanja wa bure nje, kumbe uwanjani ni mpuuzi”

Nikatamani kusema kitu ila nikaishia kukaa kimya tu.

“Wamekuone tena baada ya pale holini?”

“Hapana”

“Una uhakika?”

“Ndio”

“Hili bonge linakivunia nafasi ya baba yake kuwa mkuu wa shule nzima, ndio maana linakuwa jeuri”

“Ahaaa kumbe baba yake ni mkuu wa shule”

“Ndio, ila mimi ndio niyamkomesha kwa maana baba yake hata kwangu hazungumzi chochote”

“Unaitwa nani?”

“Mim?”

“Ndio”

“Naitwa Camila”

“Aha una jina zuri”

“Asante na wewe ulisema unaitwa nani vile?”

“Ethan”

“Sawa sawa”

Tukashuhudia goli la pili likiingia, hazikupita hata dakika mbili tukafungwa goli la tatu, na mpira ukaenda dakika za mapumziko. Bonge akwa na kazi ya kuwafokea wezake huku akitoka uwanjani akiwa amenunua sana. Wachezaji wakaka chini huku tukiwa tumemzunguka mwalimu wetu wa darasa. Mwalimu akaanza kupanga kikosi wachezaji nilio kuwa nao nje, wakaambia watacheza kipindi cha pili huku mimi peke yangu nikiwa ndio nimeachwa.

“Mwalimu mbona Ethan haujamuingiza”

“Hatuta……”

Bonge akaanza kuzungumza, ila Camila akamuonyeshea ngumi na kumfanya bonge kukaa kimya.

“Atacheza ngoja tuwajaribu na hawa wezake”

“Sawa”

Camila akanitazama huku akitabasamu na kunifanya kidogo nijawe na amani kubwa sana moyoni mwangu, kumpata rafiki ambaye kusema kweli ameanza kuwa mtetezi wangu mkubwa kutoka kwa kina bonge na kundi lake. Bonge na wachezaji wengine wakaingia katika kipindi cha pili cha mchezo huku bonge akiwa amefungw akitambaa cha uongozi wa timu. Kusema kweli mwalimu ana mpendelea bonge ila hajumudu kwa lolote uwanjani, zaidi ya kupiga piga tu kelele. Kuingia na kuingia tukafungwa goli la nne lililo mfanya mwalimu kukasirika sana.

“Mwalimu kwani Bonge ana msaada gani uwanjani?”

Camila alizungumza kwa hasira huku akimtazama mwalimu. Mwalimu akameza tu mate na kukaa kimya.

“Unamuogopa kwa sababu baba yake ni mkuu wa shule. Sasa mtoe na mimi babu yangu ni raisi”

Camila alizungumza kwa msisitozo nikamuona mwalimu akizidi kuwa mnyonge sana na akapata kigugumizi cha kufanya maamuzi. Mwalimu akamuita refa msaidizi na kumuambia kwamba anahitaji kufanya mabadiliko ya timu.

“Ila wewe unaweza au naingiza ugonjwa zaidi?”

Mwalimu aliniuliza kwa jazba kidogo jambo ambalo likaufanya moyo wangu kufedheheka kidogo.

“Nitaweza”

Nilibu kinyonge huku nikimtazama mwalimu usoni mwake. Mpira ulipo toka bonge akaambiwa kwamba anatakiwa kutoka jambo lililo mfanya bonge kukasirika sana. Nikakabidhiwa jezi yenye namba tisini na tisa mgongoni mwangu, yaani namba ya mwisho kwenye mpira.

“Jitahidi Ethan sawa”

Camila alizungumza kwa kuninong’oneza

“Sawa”

Bonge akanitazama kwa macho makali, akashindwa kunifanya chochote kwa maana amemuona Camila akiwa amesimama pembeni yangu. Alipo fika nje ya uwanja akavua kitambaa cha mkononi mwake na kukitupa chini, nikakiokota, nikataka kukivaa ila mwalimu akakataa na kuniambia nikamkabidhi kipa wetu. Nikakimbia huku nikielekea golini, nikamkabidhi golikipa kitambaa na akajifunga mkononi mwake.

‘Nicheze wapi Mungu wangu’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikiuona uwanjani ni mkubwa sana. Nikawaona washambuliaji wa darasa la kwanza wakija kwa kasi, nikajaribu kumzuia mwenye mpira, ila nikastukia kuona mpira ukipita katikati ya miguu yangu kisha akakimbilia mbele kidogo na kufunga goli la tano. Nikamtazama Camila huku mapigo ya moyo yakinienda kasi sana, woga ukanijaa. Nikimtazama mwalimu, sura yake imejaa hasira, nikiyahamishia macho yangu kwa bonge, yeye ndio usisema, naona hata pale alipo ananitukana matusi mengi sema tu siyasikii kutokana nipo mbali naye.

“Usiogope”

Mchezaji mmoja wa darasa la pili aliye nipitishia mpira wangu katikati ya miguu alizungumza huku akinipiga begani mwangu. Wezangu wawili wakachukua mpira na kuuweka katikati ya kiwanja huku mimi nikiwa nje ya dura hili kubwa. Wakanza mpira, na cha kushangaza wakanipatia mpira na wakatawanyika kuniachia kizaa zaa hichi. Nikatazama goli la wapinzani wangu, nikashusha pumzi kidogo kisha nikapiga mpira huu kwa mguu wangu wa kushoto, mpira kwa kasi huku ukielea elea hewani, ukafika golini, na golikipa wa darasa la pili akashindwa kuudaka na ukaingia nyavuni.

Nikabaki nikiwa nimeshikwa na butwaa, wanafunzi wenzangu wakaanza kunirukia huku wakishangilia, ila nikashindwa hata nifanye nini kwani sijui imekuwaje hadi mpira huo kufika golini. Nikamtazama Camila nje ya uwanja, nikamuona akininyooshea dole gumba huku akitabasamu.

“Ethan unaweza, unaweza”

Wezangu walinipa moyo huku wakitawanyika. Wachezaji wa darasa la pili wakaanza mpira, mchezaji wetu mmoja akafanikiwa kuwapokonya mpira huu na kunipasia, nikautuliaza huku nikiwaangalia wachezaji wa darasa la pili wanavyo nifwata, nikaanza kuichezesha miguu yangu kwa kuizungusha juu ya mpira, wakajaribu kuuchukua, ila nikaugusa kidogo na wakaukosa, nikaanza kukimbia kuelekea golini mwao, kila mchezaji wa darasa la pili alipo jaribu kunifwata, nilijikuta nikimtoka na akaukosa mpira huu, nilipo fika golini nikamtisha kipa kama ninapiga mpira huu kulia, jambo lililo mfanya kipa kuruka kulia, ila kwa mguu wangu wa kushoto nikaupeleka mpira huo upande wa kushoto na kuzifanya nyavu za goli la darasa la pili kutingishika. Goli hili kusema kweli, likanifanya niruke kwa furaha.

Nikakumbatiana na wachezaji wezangu kwani tuna matumaini ya kukomboa magoli matatu yaliyo salia.

‘Hii ndio nafasi ya wewe kuwa na nguvu hapa shule’

Nilimsikia rafiki yangu akiniongelesha katika ufahamu wangu wa akili.

‘Kweli’

‘Ndio, hakisha kwamba watu wanakujua wewe ni nani?’

‘Sawa’

Mpira ukaandelea, nikafanikiwa kuuchukua mpira huu na kama kawaida, nikawachenga wachezaji wa darasa la pili, nilipo fika golini, nikampatia mchezaji mwenzangu, akapiga shuti zito na tukafunga goli la tatu. Uwanja ukaanza kujaa, wanafunzi na waalimu walio kuwa wakiendelea na michezo mengine, wakaanza kuhamia kwenye huu uwanja.

“Tumebakisha goli mbili, tunaweza kujitahidi sawa”

Niliwahimiza wezangu mara baada ya kumaliza kushangilia goli letu hili. Wachezaji wa darasa la pili wakazidi kuchanganyikiwa, kwani mashambulizi yalizidi kuwaelemea, hatukumaliza hata dakika mbili, mchezaji wetu mwengine akapiga kichwa mpiwa nilio piga nikiwa pembeni ya uwanja na kufunga goli la pili.Shangwe zikazidi kurindima uwanjani hapa, watu wakasahau kama tunao cheza hapa ni watoto, ila burudani tunayo itoa kwa kweli ni ya kukata na shoka.

“Ethan, Ethan”

Mwalimu aliniita, kwa haraka nikamkibilia hadi alipo na kumshikiliza.

“Tuna dakika tano, jitahidini mukomboe”

“Tano?”

Nilimuliza huku nikimwagikwa na jasho mwili mzima.

“Ndio”

“Sawa mwalimu”

“Ethan”

Camila aliniita, akanionyeshea vidole viwili, nikamnyooshea dole ngumba kwa mkono wangu wa kulia kisha nikarudi kiwanjani. Mpira ukaanza, kutokana nimesha ujua udhaifu wa wachezaji hawa wa darasa la pili, nilicho kifanya ni kuumiliki mpira, kasi na nguvu alizo nijalia Mungu kusema kweli, zinanisaidia kuweza kuminyana nao wanafunzi hawa. Wachezaji wote wa darasa la pili wakawa wananikaba mimi na kuwasahau wezangu, nilipo fika golini kwao kwa bahati mbaya wakanichezea rafu na refa akaweka ipigwe penati. Wezangu wakaniomba nipige penati hiyo ila nikakataa, akapiga golikipa wetu, na kwa bahati nzuri akafanikiwa kufunga, ubao wa magoli ukaonyesha goli ni tano kwa tano. Nikamuona mwalimu wetu akikenua meno yote thelathini na mbili yanaonekana, akanionyeshea kwamba zimebaki dakika mbili kabla ya mpira kuisha, mpira katika kuchezwa kwa bahati mbaya ukatoka katika upande wa darasa la pili na refa akaamuru ipigwe kona. Tukakusanyika golini mwa darasa la pili, mchezaji wetu mmoja akapiga kona moja maridhwa, bila ya kuhofia kwamba nitaumia au kuvunjika, nikaruka juu na kupiga tikitaka moja nzuri na mripa ukaingia golini, na kuufanya uwanja mzima kujawa na rufaha, wezangu wakanilalia hapa chini nilipo anguka huku machozi ya furaha yakinimwagika usoni mwangu.

“ETHAN….ETHAN…..ETHA…..N”

Uwanja mzima uliimba jina langu, wezangu wakanisaidia kunyanyuka na tukarudi upande wetu. Kitendo cha darasa la pili kuanza mpira, refarii akapiga kipinga cha mwisho akishiaria kwamba mpira umekwisha. Nikamuona Camila akiingia kwa kasi uwanjani, breki ya kwanza akanirukia na kunikumbatia kwa nguvu huku akiliwa kwa furaha. Mechi tu ya kirafiki imeonekana kama mechi ya mashindano makubwa ya kugombania kombe.

“Nakupenda Ethan, nakupenda sana Ethan”

Camila alizungumza huku akiendela kunikumbatia kwa nguvu na machozi yakizidi kumiminika usoni mwake, nikajikuta nikishindwa hata kuzungumza kwani hara rafiki zake bonge walio nipiga leo bafuni, wote wakanifwata na kunikumbatia, kasoro Bonge tu yeye mwenyewe ndio amebaki nje ya uwanja huku akiwa amenuna sana na dhairi anaonyesha kwamba bado ana kinyongo na mimi.



Mwalimu wangu wa darasa akanipongeza sana huku akionekana kuto kuamini kile kilicho tokea uwanjani. Tukarudi mabwenini huku nikipongezwa na kila mwanafunzi mwenzangu. Kusema kweli tangu nije kwenye hii shule, leo ndio ambayo nimetokea kupendwa na kila mwanafunzi. Hata bafuni wachezaji wezangu hawakusita kunipongeza kwa uwezo wangu mkubwa sana nilio weza kuuonyesha katikati mchezo wa mapira na ukitegemea sisi wote bado ni watoto wadogo.

‘Unafuraha sasa?’

Niliisikia sauti ya rafiki yangu akiniongelesha.

‘Yaa nina furaha ulikuwa wapi wakati wote?’

‘Kuna mambo nilikwenda kuyafwatilia na leo nitakupeleka kwetu ukapaone’

‘Kwenu?’

‘Ndio, ili uwe mtu maarufu ni lazima ukapaone kwetu’

‘Si usiku tutakwenda?’

‘Ndio’

‘Sawa’

Nikaendelea kujifuta maji mwilini mwangu, kisha nikavaa nguo za kushindia usiku, kutoka na baridi kila mwanafunzi akavalia koti lake. Wachezaji wezangu hawakuhitaji kuniacha kila nilipo kwenda, basi wao wapo nyuma yangu. Tukapanga foleni katka bwala la chakula, sifa zikazidi kuniandama hadi kwa wadada wakubwa wa madarasa mengine. Kitendo hichi dhairi kikaanza kumkosesha amani Camila, akanifwata katikati ya wadada hawa wanao niuliza mambo mawili matatu huku nikiwa nimeshika sahani yanu ya chakula, akanichukua na tukatafuta meza yetu iliyo jitenga na tukaka.

“Tukae hapa wenyewe”

Camila alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.

“Mbona kama umekasiria ikiwa leo ndio siku ya furaha?”

“Sitaki kukuona na wale wadada”

“Kwa nini?”

“Sitaki tu”

“Mmmmm”

Mlinzi wa Camila akaleta chakula kisha wakasimama mbali kidogo na meza hii.

“Hawa walinzi wanakulinda muda wote?”

“Ndio, ila ninapo kwenda kulala huwa waniacha na wanakuja kuchukuliwa na asubuhi wanakuja tena”

“Wanachukuliwa na kina nani?”

“Hawa ni usalama wa taifa, hivyo lazima wakaripoti makao makuu”

“Ahaa”

“Ila leo Ethan umefanya jambo moja ambalo ni la kushangaza sana”

“Jambo gani?”

“Si kufunga magoli matatu na kusaidia timu kutoka nyuma magoli matano hadi kushinda. Nakuhakikishia ukiwa hivyo basi hadi unakuwa mkubwa basi vilabu vikubwa hapa Ujerumani vitawahi kukununua”

“Hahaaa kweli?”

“Kweli vile na ninapenda kukuambia jambo moja”

“Jambo gani?”

Camila akaka kimya kidogo huku akinitazama usoni mwangu.

“Zungumza”

“Ethan nina kupenda, nataka uwe mchumba wangu”

Moyo ukanistuka sana, kwani kwa umri wangu huu ni jambo zito sana kusikia kwamba nina pendwa na mtu anataka kuwa mchumba wangu, ikiwa hata maana ya mapenzi sifahamu.

“Ethan natambua kwamba una shangaa mimi kukuambia hivyo, ila huo ndio ukweli wa moyo wangu, nina kupenda sana, sipendi ninapo kuona na wasichana wengine nina jisikia wivu moyni mwangu”

“Ila Camila sisi bado ni watoto, tutawezaje kuhimili mikiki mikiki ya mapenzi yetu?”

“Si tutakua wakubwa, kwani kila siku tutabaki kuwa hivi. Lazima tuwe wakubwa na tukiwa wakubwa basi penzi letu litazidi kuwa kushamiri, tutafunga ndoa na kuzaa watoto wetu”

Nikazidi kushanga sana kumuona mtoto mdogo kama Camila akiwa na ujasiri wa kuzungumza mambo ambayo kwa umri wetu, endapo unazungumza tena ukiwa nchini Tanzania, basi ni lazima utachapswa sana na mzazi pale atakapo sikia kuhusiana na mazungumzo haya.

“Camila, huku kwenu unyanyasaji wa watu kama sisi ni mkubwa, nina ogopa?”

“Ethan hilo nitalichukulia uangalizi, hakuna mtu ambaye atakunyanyasa. Babu yangu ni raisi, babu yangu ana majeshi na ananipenda sana babu yangu, hivyo chochote ninacho mueleza ananisikiliza, na hakuna wa kukutisha sawa Ethan”

Camila alizungumza huku akivua gloves alizo vaa mikononi mwake kwa ajili ya kuzuia barini, akanishika mkono wangu wa kulia huku akinitazama usoni mwangu.

“Ethan nitakulinda kwa namna yoyote ile, nakupenda Ethan”

Camila alizungumza huku machozi yakimlenga lenga usoni mwake, hapa ndipo nikatambua kwamba jambo analo lizugumzia ana limaanisha kutoka moyoni mwake. Kutokana nina hitaji usalama wa maisha yangu ya hapa shuleni, sikuwa na budi zaidi ya kumkubalia. Camila akatabasamu, hapa ndipo nikazidi kuuona uzuri wake, japo ni mzungu ila amejaliwa uzuri na ujasiri mkubwa wa kuweza kuhitaji kumiliki chochote anacho kihitaji yeye.

Tukamaliza kupata chakula cha usiku na tukarudi mabwenini kwetu, huku wasichana wakielekea kwenye mabweni yao. Leo stori za wanafunzi wote ni kuhusian ana mimi pamoja na timu yangu, huku wengine wakijilaumu ni kwa nini kocha hakunianzisha mapema katika mechi iliyo pita.

“Umesha wahi kucheza mpira kabla ya leo?”

Mwanafunzi mwezangu aliniuliza.

“Hapana”

“Kweli?”

“Ndio haki ya Mungu, leo ndio siku ya kwanza kucheza mpira”

“Aisee unakwenda kuwa zaidi ya Messi na Christian Ronaldo”

Mwanafunzi huyo aliendelea kunimwagia sifa kedekede. Muda wa kulala ulipo fika, mlezi wa bweni letu akatuomba kila mwanafunzi aingie kwenye chumba chake na kulala. Mimi na rafiki zangu watatu tukaingia kwenye chumba chetu cha kulala, siku zote za nyuma sikuwa na maelewano nao mazuri, kutokanana rangi yangu ya mwili kwamba ni muafrika, ila leo hii wamekuwa ni watu ambao wana nisikiliza kwa kila kinacho kizungumza.

Tukaendelea kuzungumza mambo mbalimbali yanayo husiana na maisha ya hapa shuleni na familia zetu, baada ya mdua kidogo tukajikuta tukipitiwa na isingizi na watu wote tukalala usingizi fofofo.

‘Ethan’

Niliisikia sauti ya rafiki yangu ambaye hadi leo hajanitambulisha jina lake.

‘Naam’

‘Amka’

Rafiki yangu huyu alizungumza, taratibu nikanyanyuka kitandani, katika hali ambayo kwa binadamu wa kawaida hawezi kuifahamu, tukaanza kuondoka katika eneo hili huku kwa upande wangu nikiona ni jambo la kawaida sana.

‘Leo utaweza kuniona mimi na familia yangu’

‘Sawa, ila kwa kuna maswali nahitaji kukuuliza?’

‘Uliza?’

‘Hivi hamtishi nitakapo waangali?’

‘Hahaaa…hatutishi, kwa nini umefikiria kwamba tunatisha?’

‘Kwa maana kila siku ninaona kivuli chako na kama hivi tunavyo elea hewani, nina hisi uwepo wako tu ila sikuoni sura wala mwili wako’

‘Usijali utaniona tu’

‘Kweli?’

‘Ndio’

Tukafika baharini, maji yakaanza kuzunguka kama kimbunga kikubwa sana na kusababisha shimo kubwa sana, tukaanza kushuka kwenye shimo hili lenye maji, kila kitu kinacho tokea kusema kweli kina nishangaza. Tukafika katika mji mmoja mkubwa sana ambao watu wake ni tofati na binadamu. Watu hawa wengi wao wanatembea hewani na si ardhini.

‘Maisha ya huko usije ukamuelea mtu wa aina yoyote na siku ambayo utazungumzia juu ya haya mambo basi maisha yako yatakuwa ni ya shida sana umenielewa Ethan?’

‘Ndio, naweza kuluuliza?’

‘Uliza?’

‘Kwa nini watu hawa wanatembea hewani na ni wazuri sana kuliko hata binadamu?’

‘Huu ni ulimwengu wa majini, kuna majini wabaya na majini wa zuri. Sisi ni majini wazuri’

Wasiwasi ukaanza kunijaa kidogo.

‘Usijawe na wasiwasi wowote, hadi kufika huku ujue nimekuchagua na tunataka uwe muwakilishi wetu mzuri duniani’

‘Muwakilishi wa mambo gani?’

‘Kadri siku zinavyo zidi kwenda na unavyo zidi kukua ndivyo jinsi utakavyo weza kufahamu ni uwakilishi gani ambao sisi tunauhitaji kwako’

Tukaingia kwenye jumba moja kubwa ambalo katika kuona kwangu majengo dunia, jengo hili sijawahi kuliona. Rafiki yangu huyu akaonekana umbo lake. Nikabaki nikiwa nimejawa na mshangao kwa maana ni kijana mdogo kama mimi na ni mzuri sana ila ana sauti nzito sana.

‘Mbona wewe ni mdogo!!!?’

‘Yaa ulihisi mimi ni mkubwa sana’

Alizungumza kwa sauti nyinine ambayo ni tofauti na sauti ambayo anazungu akiwa katika mwili usio onekana. Tukaanza kutembea kwenye kordo ya jumba hili, wasichana wazuri na wanaume wazuri kila ambao ana kutana nao wana muinamishia kichwa chini huku wengine wakimpigia na magoti chini kabisa.

“Kwa nini wana kuinamia?”

Nilimuuliza huku tukizidi kusonga mbele.

“Mimi ni mfalme wa huku chini, baba yangu alifariki miaka miachache iliyo pita”

“Ngoja kwanza una taka kuniambia kwamba nyinyi muna kufa?”

“Ndio tunakufa, ila kuishi kwetu sio kama wa binadamu, miaka kumi hamsini mia. Ila sisi tunaweza kuishia kuanzia miaka elfu kumi na ndio tunaweza kufa”

“Heee”

Tukaingia kwenye moja ya ukumbi, ambao wote umesakafiwa kuanzia kuta, nguo kwa kutumia dhahabu. Tukaendelea kutembea hadi kwenye kiti kikubwa cha dhahabu na akaka na wote waliomo ndani ya ukumbi huu wakainama chini na kumsujudia. Akapiga kofi moja wakayanyuka na kwa ishara akawaomba watokea ndani humu na tukabaki sisi wawili.

“Hawa ni kina nani?”

“Ni wafanyakazi wangu ambao ninaweza kuwatuma sehemu yoyote ulimwenguni na wakaniletea chochote nitakacho kihitaji”

“Chochote kile?”

“Yaaa njoo ukae”

Alizungumza huku akinionyesha kiti kilichopo pemeni ya kiti cheke, ambacho nacho kimetengenezwa kwa madini ya dhabu.

“Huku ni pazuri sana”

“Yaa ni pazuri, alafu umesahau kuniuliza jina langu”

“Ndio. Unaitwa nani?”

“Nina itwa Ethan kama wewe”

“Acha kunitania bwana?”

“Niamini mimi, nina itwa Ethan, ndio maana niliamua kuwa rafiki yako toka siku tu ulipo saidia wa wale wazee”

“Kwa hiyo ulikuwa una nifwatilia?”

“Ndio, siku hiyo nilikuwa ninapita kwenye matembezi yangu ya kila siku, nikakuona ukiwa upata tabu, nilitaka kuwadhuru wale walio kuwa wakikupa tabu, ila nikawaona hawana la maana, walipo kutupa basi nikawa pamoja na wewe”

“Ngoja kwanza, ni kina nani ambao walinitupa?”

“Kwa sasa Ethan sio muda sahihi wa wewe kuweza kuwafahamu watu hao, ila jambo la msingi ni kuhakikisha kwamba una pata kile unacho kihitaji kisha hayo mambo mengine kadri jinsi tunavyo zidi kwenda ndivyo jinsi utakavyo zidi kuyafahamu”

“Sawa nimekuelewa”

“Wewe ndio binadamu wa kwanza kuwa rafiki yangu.Ila ninakuomba usije ukanisaliti siku hata moja, ukinisaliti kila kitu kitamu kwako nitakibadilisha na kitakuwa kichungu na urafiki wangu mimi na wewe utakufa sawa”

Ethan mwenzangu alizungumza kwa ukali kidogo na msisitizo, nikatingisha kichwa nikimaanisha kwamba nimemuelewa anacho kizungumza.

“Unahitaji nguvu si ndio?”

“Ndio”

Kwa ishara Ethan akaniomba nisimame mbele yake, akaniamrisha nipige magoti mbele yake na nikapiga kweli magoti. Akaniweka mkono wake wa kulia kichwani mwangu, mwili wangu mzima nikahisi kuna nguvu fulani inaniingia, Ethana akaendelea kunipatia nguvu hadi mwili wangu ukaanza kutetemeka, na mwishowe nikajikuta nikianguka chini na kupoteza fahamu.



“Ethan, Ethan”

Niliisikia sauti ya marafiki zangu wakiniamsha kutoka usingizini, nikafumbua macho yangu na kumuona rafiki yangu akiwa amepanda ngazi za kitanda changu huku akinitazama.

“Kumepambazuka, amka tuwahi darasani?”

“Ni saa ngapi?”

“Sa moja kasoro asubuhi”

Nikakurupuka kitandani kwa haraka sana, kwani muda wa kuamka siku zote ni saa kumi na mbili asubuhi. Nikakimbilia bafuni huku nikiwa nimejifunga taulo, nikaingia bafuni na kuanza kuoga haraka haraka huku nikijaribu kufikiria nimeruidije rudije hapa chuoni. Ila sikuhitaji kuliweka sana jambo hili akilini mwangu kwa maana ni mara nyingi huwa nina toka na Ethan mwenzangu ambaye jana niliweza kumtambua jina lake na muonekano wake, na kisha tunarejea sehemu anapo nitoa. Nikarudi chumbani, nika wakuta wezangu wamesha niandalia nguo zangu za kuvaa jambo ambalo kwa kweli lime nishangaza sana.

“Asanteni”

Nilizungumza huku nikianza kuvaa nguo zangu, nilipo hakikisha kwamba nimemaliza, kuvaa na viatu tukatoka chumbani humu na kuelekea kwenye kiwanja ambacho tunakusanyika wanafunzi wote kila asubuhi na baada ya hapo tunaelekea kwenye madarasa yetu. Mkuu wa chuo akatutangazia kuhusiana na kuanzisha ligi ya mpira kwa shule nzima kuanzia msingi hadi sekondari, msindi atakaye patikana katika shule ya msingi atacheza fainali na mshindi atakaye shida katikashule ya sekondari. Furaha ikanijaa sana kwani hii ndio nafasi yangu ya pekee ya kuzidi kuonyesha kipaji changu cha mpira. Tukaruhusiwa kutawanyika darasani, kwa haraka Camila akanifwata sehemu nilipo simama na rafiki zangu, nikajitenga pembeni na rafiki zangu.

“Vipi mpenzi wangu”

Camila alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.

“Salama niambie”

“Safi, nimekuletea zawadi, usiifungue nenda kaifungue darasani kwako”

Camila akanipatia kiji boksi kidogo alicho kifunga vizuri na kuandika jina langu juu ya kiboksi hichi.

“Kuna nini?”

“Wewe nenda kafungulie darasani kwako”

Camila alinisisitizia na akaondoka huku akiwa ameongozana na kundi la rafiki zake. Nikiwa rafiki zangu watatano, tukaelekea darasani kwetu, ubaya mimi na Camila tupo madarasa mawili tofauti. Nikaka kwenye dawati langu, kwa haraka nikafungua kiboksi hichi na kukuta karatasi nyeupe iliyo kunjwa vizuri, kwa haraka nikaifungua, sikuamini macho yangu baada ya kukuta picha yangu ya jana nilipo funga goli la tikitaka, ikiwa imechora vizuri. Nikayashusha macho yangu hadi kwenye jina la mchoraji na nikakuta ni Camila.

“Ethan ni nani amekuchorea hivyo?”

Binti mmoja aliniuliza huku akichungulia picha yangu, kwa haraka nikaikunja na kuiweka katika mfuko wa kaptula yangu.

“Hamna kitu”

Nilimjibu kwa ufupi tu, akiangia mwalimu wa hesabu, somo ambalo kusema kweli silipendi hata kuliona, japo nipo darasa la kwanza ila kusema kweli lina nishinda nahata ufuliji wake kwa upande wangu si mkubwa kivile.

Mwalimu akaendelea kufundisha huku akilini mwangu nikiwa nina fikiria picha niliyo pewa zawadi na Camila mwanamke ambaye taratibu ana anza kuuteka moyo wangu.

Kitu nilicho weza kukigundua kwenye nchi hii, watu wana uhuru wa kueleza hisia zao kwa wanao wapenda haijalishi umri ua jinsi. Ni tofauti na bara letu la Afrika hususani katika nchi yangu ya Tanzania, ni marufuku watoto kupenda hadi wafikishe miaka kumi na nane au watoke nyumbani kwa wazazi.

“Ethan njoo ujibu swali hili ubaoni?”

Nikastuka sana baada ya mwalimu kunigusa begani mwangu, nikatazama swali lenyewe ubaoni, ni swali linalo husiana na maswala ya kuzidisha, hesabu ambazo kusema kweli zizipendi. Darasa zima wakanitazama, mwalimu akanikabidhi chaki, taratibu nikanyanyuka huku nikiwa nimejawa na wasiwasi mwingi sana.

‘Unashindwa wapi, waza’

Niliisikia sauti ya Etathan akiniongelesha. Nikasimama ubaoni, nikafikiria kidogo na nikaweza kupata jibu la swali hili, nikalijaza na mwalimu akawaamuru watu kunipigia makofi kwa maana nimepatia swali lake, jambo lililo anza kunipa faraja na kulipenda somo la hesabu.

***

Siku ya mapumziko ikafika, bibi Jane Klopp akafika shuleni hapa kunitembelea, kama ilivyo kuwa kawaida kwa wazazi wenye wanafunzi wengine kuja kunitembelea. Nikasalimiana naye kwa furaha huku tukikumbatia.

“Hongera sana Ethan”

“Hongera ya nini tena mama?”

“Nimesikia sifa zako kutoka kwa mwalimu wako wa mpira na amenitumia video hii ukicheza mpira”

Bibi Jane Klopp akanionyesha video iliyo rekodiwa na simu, nikiwa ninacheza mpira.

“Ukiendelea hivi nakuhakikishia kwamba utakuwa ni mchezaji mzuri sana mwanangu”

“Sawa mama, nakuahkikishia kwamba ninatakuwa mchezaji mzuri sana, na nitafanya kila liwezekanalo kuliweka jina la baba juu”

“Hahaaa safi sana, nimefurahi kusikia hivyo, nitakutengenezea jezi yako iliyo andikwa E.KLOPP au unasemaje”

“Yaa itakuwa ni nzuri sana mama. Vipi dada na baba wanaendeleaje?”

“Wanaendelea vizuri, dada yako amesha anza kutembea, nimewaacha leo wakielekea hospitalini kwa vipimo vya mwisho”

“Aha sawa sawa, atapona”

“Ni kweli atapona Mungu ni mwema”

Nikamuona Camila na walinzi wake wakika katika benchi hili tulilo kaa mimi na bibi Jane Klopp katika bustan hii. Camila akamsalimia bi Jane Klopp kwa heshima zote. Nikamtambulisha Camila kwa bibi Jane Klopp.

“Ninamfahamu huyu binti, mama yako si Priscar”

“Ndio bibi”

“Yaa wewe na mama yako ni marafiki sana. Ninafurahi sana kuona umekuwa rafiki wa mwanangu hapa shule, kikubwa hakikisheni kwamba muna zingatia masomo. Sawa”

“Sawa mama”

“Vipi mama yako amekuja kukutembelea leo?”

“Hapana, takuja babu baadae”

“Ahaa, ndio maana nimeona ulinzi umeimarishwa hapa”

“Ndio bibi”

Tukaendelea kuzungumza na bibi Jane Klopp hadi wakati wa mchana na tukapata chakula pamoja kisha akatuga na kuondoka.

“Babu yako atakuja muda gani?”

“Kwenye saa tisa hivi”

“Ila si raisi baba yako?”

“Ni raisi kwa watu wengine ila kwangu mimi ni babu yangu, nimemuomba aje kunitembelea na atakuja”

“Sawa, ngoja nipeleke hizi zawadia alizo niletea mama, bwenini”

“Twende wote”

“Wee Camila umeona wapi bweni la wavulana mukaingia nyinyi wasichana”

“Wewe twende”

“Mmmmm”

“Tena lete nikusaidie kubeba mfuko huo”

Camila akanisaidia kubeba mfuko mmoja mweusi. Tukaanza kutembea taratibu kuelekea bwenni huku walinzi wake wakitufwata kwa nyuma. Tukafika kwenye mlango wa chumba ninacho lala, nikamuomba aweze kunisubiria nje, ila akanikatalia, na akawaamuru walinzi wake wasubiri nje na tukaingia wote ndani.

“Camila ila tunavunja sheria za shule”

“Babu yangu anakuja leo, walimu wote akili zao zipo kwenye ugeni huu wala usihofie, hakuna atakaye jua hili”

Camila alizungumza huku akiufunga mlango kwa ndani. Mapigo ya moyo yakazidi kunienda kasi kwnai kusema kweli katika vitu ninavyo ogopa ni katika kuvunja sheria ya shule na isitoshe bibi Jane Klopp hata leo ametoka kunisisitizia hili. Camila akaitazama picha aliyo nipatia kama zawadi nikiwa nimeibandika ukutani pembeni ya kitanda changu.

“Nilikupatia”

“Aliye chora ni wewe?”

“Ndio ni mimi, mama yangu ni mchoraji mahiri sana na nimerithi kipaji chake”

“Hongera sana”

Camila akanisogela sehemu nilipo simama, akanikumbatia kwa nguvu.

“Ethan ninakupenda sana natamani miaka iende tukue, tuanze kuishi pamoja”

“Usijali, tutafikia tu umri wa kukua”

Taratibu Camila akanitazama usoni mwangu, kisha akayafumba macho yake huku akiusogeza mdomo wake karibu yangu, jambo lililo nishangaza sana na kunifanya nitetemeke mwili mzima hadi nikahisi haja ndogo inataka kunitoka. Midomo yetu ikagusana, hapo ndipo nikahisi ubaridi mkali ukikatiza mwilini mwangu kutoka utosini hadi kwenye nyanyo zamiguu yangu. Kitendo cha Camila kuupenyesha ulimi wake katikati ya lipsi zangu na kugusana na ulimi wangu, nikahisi msisimko ulio fanya uume wangu kusimama. Mlango ukagongwa, Camila akaniachia kwa haraka huku macho yakiwa yamelegea.

“Madam, raisi anakaribia kufika shuleni, unaweza kutoka sasa”

Tuliisikia sauti ya mlinzi wake mmoja. Camila akashusha pumzi kwa nguvu.

“Nina kuja”

Camila alijibu kwa sauti ya ukali, kisha akanibusu shavuni mwagu.

“Nakupenda Ethan”

“Ninakupenda pia Camila.”

“Twende ukamuone babu yangu”

“Ahaa…siku nyingine nitamuona”

“Twende bwana”

“Hapana Camila”

Nilizungumza huku nikiushika uume wangu nikiuweka vizuri kwenye suruali yangu hii ya kushindia niliyo ivaa. Camila akanitazama kwa muda kisha akatabasamu, akanibusu mdomoni kisha akatoka ndani humu na kuniacha nikiwa hakika hali ya mawazo yangu, kwani hali ninayo jihisi mwilini mwangu, leo hii ndio mara yangu ya kwanza. Nikajilaza kiyandani mwangu huku nikiwa bado siamini.

‘Hahaaaha…….’

Nilisikia kicheko cha Ethan ndani ya chumba hichi, nikaka kitako kitandani na kumkuta akiwa amekaa kitanda cha mbele yangu.

“Mbona umekuja saa hizi, watu si watakuona?”

“Hakuna ambaye anaweza kuniona zaidi yako. Mbona umeshindwa kufanya chochote kwa mchumba wako?”

“Ethan kumbuka mimi bado ni mtoto na mambo hayo wala siyaelewi”

“Hahaaa…utataka kuyaelewa?”

“Hapana kwa muda huu acha kwanza nisome”

“Sawa, ila kuwa makini sana na huyu binti”

“Makini kivipi?”

Mlango ukafunguliwa akaingia rafiki yangu mmoja ambaye analala chumbani humu.

“Mbona unazungumza peke yako au nimesikia vibaya?”

“Utakuwa umesikia vibaya.”

“Twende tukampokee raisi?”

“Najisikia vibaya nahitaji kupumzika kidogo”

“Ahaa….sawa, kwa maana nilikutafuta kule nikahisi kabisa kwamba utakuwepo huku”

“Vipi wazazi wako wamekuja?”

“Ndio wamekuja na wamesha ondoka”

“Sawa”

Rafael akatoka chumbani humu na kuniacha mimi na Ethan ambaye ni jini asiye onekana kwa watu wengine zaidi yangu mimi peke yangu.

“Ethan umesema kwa nini niwe makini na huyu binti”

“Anakupenda sana, sasa kukupenda kwake, kusije kukakuletea matatizo katika masomo yako na amani yako”

“Kivipi?”

“Ni mapema sana kuzungumzia mambo ya miaka mitano ijayo mbeleni, kwa sasa endeleeni kula maisha”

Ethan alizungumza huku akicheka.

“Hivi jana ilikuwae?”

“Imekuwa kama ilivyo kuwa au?”

“Mbona nilijikuta nikiwa kitandani?”

“Yaa nguvu ambazo nimekupatia utazitumia kwa miaka ijayo.”

“Miaka mingapi ijayo?”

“Ohooo Ethan”

“Nini?”

“Angalia mlangoni”

Nikatazama mlangoni, sikuona kitu chochote, nikageuka kumtazama katika sehemu ambayo alikuwa amekaa, ila sikumuona, nikastukia mlango ukifunguliwa, akaingia mzee mmoja aliye valia suti nzuri huku akiwa ameongozna na walinzi huku mkono wake wa kulia akiwa ameshika Camila ambaye usoni mwake ana mwagikwa na machozi. Nikanyanyuka kwa haraka kitandani na nikamsalimia mzee huyu kwa heshima sana, ila sura yake ikaonyesha kukasirika sana, na kwa haraka nikaweza kumtambua kwamba huyu ndio raisi wa hapa Ujerumani kwa maana picha yake ipo katika ofisi ya mkuu wa shule na waalimu wengine.



ENDELEA

“Wewe ndio kijana unaye itatiza akili ya mjukuu wangu?”

Mzee huyu alizungumza kwa ukali sana hadi mimi mwenyewe nikaanza kutetemeka huku machozi yakianza kunilenge lenga.

“Ninakuonya mtoto, kaa mbali na mjukuu wangu la sivyo hii nchi utaiona mbaya, na wewe umekuja shule kusoma na si kuingia ingia kwenye mabweni ya wanaume umenielewa?”

Camila akatingisha kichwa huku akiendelea kumwagikwa na machozi usoni mwake. Mzee huyu akanitazama kwa muda kidogo kisha wakatoka ndani humu na walinzi wake. Mwalimu wangu wa darasa akaingia huku akiwa amejawa na sura ya huzuni.

“Ethan”

“Naam”

Niliitikia kwa sauti ya unyonge sana huku nikimtazama mwalimu wangu huyu ambaye ana nipenda kutokana na kipaji changu cha mpira uwanjani.

“Una mahusiano na huyu binti?”

Mwalimu aliniuliza kwa sauti ya upole sana huku akiwa amekaa kitandani, kwa uoga nilio nao nikajikuta nikishindwa hata kuzungumza zaidi ya kuanza kulia. Taratibu mwalimu akanivuta jaribu yangu na kunikumbatia na kuanza kunibembelea kwani habari hii ikifika kwa bibi Jane Klopp na mume wake sijui watanichukuliaje.

“Usiwe karibu na yule binti sawa”

“Sawa mwalimu, ila ni rafiki yangu tu wa kawaida?”

“Ndio nina litambua kwa umri wako huwezi kuwa na mahusiano ila muheshimiwa alikuhisi tu vibaya, ila nakuomba usipende kuwa naye karibu sihitaji kukupoteza kwenye darasa langu”

“Sawa mwalimu”

Mwalimu akaniachia huku akinitazama usoni mwangu. Akaniomba niweze kujipumzisha na nisitoke ndani humu hadi kesho. Mwalimu alipo ondoka rafiki zangu wakingia ndani ya chumba hichi huku nao wakiwa wanahitaji kufahamu ni kitu gani ambacho kimetokea hadi raisi kunifwata humu bwenini. Kwa mtazamo wa haraka haraka wengi wao wanahisi kwamba raisi amekuja kunipongeza kwa kufanya vizuri kwenye mechi yangu ya kwanza tu.

“Ethan unazidi kuwa maarufu”

Wezangu walizidi kunipongeza huku wakiwa wamejawa na fur asana, ila laiti kama wangefahamu kwamba nimetoka kufokewa tena na mkuu wa nchi yao wala wasinge zungumza lolote juu yangu.

***

Umaarufu wangu katika shule hii ukazidi kupanda siku hadi siku. Michuano ya mpira madarasa ya shule hii ya msingi yakazidi ninifanya nizidi kuwa kipenzi cha wanafunzi na waalimu wengi. Kwani nikiwa kama kapten wa timu yangu, ya darasa la kwanza, niliweza kuingoza timu yangu katika kila ushindi tulio upata katika mechi za madarasa tulizo kutano nayo. Katika safu ya ufungaji, niliongoza kwa magoli ishirini na sita huku anaye nifwatia akiwa na magoli kumi. Katika kipindi chote sikuhitaji kukaa karibu na Camila na kila nilipo muona ana kuja nilipo kwa ajili yangu, nilifanya kila ina ya mbinu kuhakisha kwamba nina mkwepa.

“Ethan”

Niliitwa na msichana mmoja tukiwa uwanjani tunajiandaa na mechi ya kucheza na darasa la sita.

“Ndio”

“Kuna ujumbe wako hapa”

“Kutoka kwa nani?”

“Wewe chukua”

Msichana huyu alinipa ujumbe huu, nikataka kuusoma ila mchezaji mwenzangu aka nizuia kwa maana tumebakisha dakika chache sana kabla ya kuingia uwanjani. Ujumbe huu nikauingiza kwenye soksi zangu za mpira kisha nikaingia uwanjani. Mwalimu akaniita kwa ajili ya kunipa maelekezo yake kama kocha.

“Una muona yule mwenye macho ya blue kiasi?”

Mwalimu alizungumza huku akinionyesha mchezaji wa darasa la sita.

“Ndio”

“Yule ni beki wao, na anacheza rafu anaweza hata kukuvunja. Hakikisha kwamba unakuwa makini naye sawa”

“Sawa mwalimu”

“Ushindi ni muhimu, kumbuka tuna mechi moja mbeleni, tukishinda hii ya robo fainal, najua tutakao kutana nao nusu nilazima tutawafunga na tutaingia fainali”

“Sawa kocha”

Nilizungumza huku nikiangaza angaza macho yangu katika kumuangalia ni wapi alipo Camila, ila nikashindwa kabisa kumuona jambo lililo nipa wasiwasi mwingi sana, japo ninamkwepa ila moyo wangu una niuma sana. Nikamuona mlinzi mmoja wa Camila akifika katika eneo hili kwa kasi sana, akamnong’oneza mwalimu jambo amalo hata mwalimu mwenyewe akaonekana kustuka kidogo. Mwalimu akanitazama kwa sekunde kadhaa kisha aka ninong’oneza.

“Nakuomba uongozane na huyu mlinzi kuna jambo la muhimu sana limetokea, ila hakikisha kwamba unatumia kila mbinu unalitatua na unarudi hapa kiwanjani sawa”

“Sawa”

Nikavua kitambaa cha muongozaji wa timu(capten) na nikanza kukimbia na mlinzi huyu, jambo ambalo kidogo likawastua mashabiki walio weza kuliona tukio hilo. Tukakimbilia hadi kwenye mabweni ya wasichana na nikawakuta baadhi ya waalimu na wazazi wa Camila wakiwa chini ya gorofa hili huku juu kabisa akiwepo Camila mwenyewe akihiyaji kujirusha kutoka gorofani hapo ili afe. Hapa ndipo nikawazia juu ya ujumbe ambao nilipatiwa na sikuusoma.

“Wewe ndio Ethan?”

Mama Camila aliniuliza huku machozi yakimwagika usoni mwake.

“Ndio ni mimi”

“Ninakuomba umsaidie mwanangu, nakuomba mwanangu ana kuhitaji wewe tafadhali nakuomba sana kijana”

Nikasimama katika sehemua mbayo Camila ambayo anaweza kuniona, nikamtazama.

“Camila……Camil”

Niliita kwa sauti ya kuu na Camila akanitazama.

“Panda juu ukazungumze naye tafadhali”

Baba Camila alizungumza huku naye akionyesha dhairi kwamba ana wasiwasi mkubwa sana. Nikaanza kupandisha ngazi za gorofa hili huku nikikimbia, nikafika gorofa ya nane na nikapanda juu kabisa alipo Camila, nikamakuta akiwa amesimama kwenye ukingo wa gorofa hili na endapo atafanya mchezo kidogo basi anaanguka chini na kufa.

“Camila, kwa nini unataka kufanya hivyo mpenzi wangu”

“Ethan kaa mbali na mimi, hunipendi”

Camila alizungumza kwa ukali sana.

“Ninakupenda Camila, nina kuhitaji mpenzi wangu”

“Kwa nini ushindwa kupigania penzi letu. Ninakufwata ila unanikimbia kimbia, ni maisha gani ambayo unanifanyia lakini eheee?”

Camilia alizungumza huku akilia sana, kwa umri ambao tunao hakika haistahili kwa sisi kuwa na mapenzi ya namna hii, kusema kweli Camila ana nipenda hadi anaamua kutaka kujiua kwa ajili yangu.

“Hapana Camila, nina ogopa. Baba yako anaweza kunidhuru, je unataka nife ehee?”

“Acha nife mimi kama unaogopa kufa”

“Hapana Camila, sihitaji ufe. Nina kuapia kwa mwenyezi Mungu kuanzia leo wewe ni wangu, hakuna ambaye atatutenganisha, nife mimi au ufe wewe, ila wewe ni wangu Camila”

Nilizungumza huku machozi yakinimwagika usoni mwangu, nikaanza kutembea taratibu huku nikimfwata Camila alipo simama.

“Camila na kuomba usifanye hivyo mpenzi wangu, nakuomba sana.”

“Ethan wewe hunipendi una nidanganya”

“Nakuapia haki ya Mungu nipo tayari kwa lolote, nina kupenda sana Camila wangu”

Niliendelea kuzungumza huku nikipiga hatua za taratibu hadi nikafanikiwa kufika sehemu alipo simama Camila, taratibu nikampatua mkono wangu wa kulia huku nikiendelea kumtazama usoni mwake.

“Camila, nipo tayari tukue pamoja, tuje kuishi pamoja na kuzaa watoto pamoja. Nitakuepeleka kwetu Tanzania, ukaona mazingira mazuri ya nchi yetu nakuomba sana Camila wangu tafadhali.

Camila akanitazama kwa macho yake mazuri, akashusha pumzi taratibu.

“Una niahidi nini?”

“Tayari nimesha kuahidi mengi mpenzi wangu”

“Nataka kusikia upya”

“Nakuahidi kuwa na wewe, nakuahidi kuishi nawe, nakuahidi kukupeleka kwetu Tanzania, nakuahidi kupigania penzi letu, nina kupenda sana mpenzi wangu”

“Upo tayari kusimama mbele ya babu yangu na kumuambia kwamba una nipenda?”

“Ndio nipo tayari”

Nilijibu ili maradi kumridhisha, ila kusema kweli sina ujarisi wa kusimama mbele ya mzee huyu mkali sana, na nimuambie kwamba nina mpenda mjukuu wake. Camila akanivuta mkono wangu na kuanza kushuka kwenye ukingo huu wa gorofa. Tukakumbatiana kwa nguvu, Camila akaanza kunibusu mdomoni mwangu bila ya kujali kwamba tupo katika eneo la shule.

“Nisikilieze mpenzi wangu, uwanjani mechi imesha anza, ninakuomba twende ukanishangilie mume wako”

“Kweli mpenzi wangu?”

“Ndio”

“Na leo nataka ufunge magoli matano mpenzi wangu”

“Sawa, kwa ajili yako nitafunga”

“Nakupenda sana Ethan”

“Nakupenda pia Camila wangu”

Mlango wa eneo la huku juu ukafunguliwa, akaingia baba mama Camila kisha akafwatia mke wake pamoja na walinzi wao. Wote wakashangaa ni ushawishi gani ambao nimeufanya kwa binti yao hadi kugairi kujiua.

Camila akaniachiana kukumbatiana na wazazi wake.

“Tunashukuru sana kijana”

Alizungumza baba Camila huku akinitazama usoni mwake.

“Sawa sawa mzee”

“Wazazi wangu, naomba mumuambie babu, nina mpenda Ethan, ninataka awe ndio mwanaume wa maisha yangu, sijali ni muafrika au ni mweusi na wala sijali utoto wetu, ila ninampenda, naomba musikilize hisia zangu wanazai wangu”

Camila alizungumza huku machozi yakiendelea kumwagika. Walimu nao wakafika katika eneo.

“Tutamueleza na sisi ndio wazazi wako, sisi ndio wenye maamuzi juu yako na si baabu yako. Tupo tayari uwe na huyo kijana kwa maana hatujaona ubaya wowote kwake kwanza ni handsome boy”

Mama Camila alizungumza huku akinikonyeza. Nikatabasamu huku nami nikiwa nimejawa na furaha.

“Kweli mama?”

“Asilimia mia moja”

“Asante mama na baba nina wapenda sana”

“Tuahidi hauto fanya hili jambo tena?”

Baba Camila alizungumza huku akimtazama mwanaye usoni

“Sinto lifanya nina waahidi wazazi wangu ila mukinitenganisha na Ethan kwa namna yoyote basi nitajiua”

Camila alizungumza kwa msisitozo na wazazi wake wakaka kimya.

“Mpenzi wangu ni mchezaji mpira, na timu yake ipo uwanjani, twendeni tukamshangilie”

“Sawa twendeni”

Tukaondoka juu ya gorofa hili na kuelekea uwanjani. Tukiwa karibu ya uwanjani tukasikia shangwe kubwa ambazo zikanifanya nikimbilie uwanjani. Nikatazama ubao wa magoli, nikaona timu yangu ikiwa imefungwa goli mbili bila na goli hili la pili ndio limetoka kuingia muda si mchache. Mwalimu alipo niona akatanasamu sana kwani timu inacheza kwa kuto kujiamini na nina amini kwamba wachezaji wezangu watakuwa wakijiuliza ni wapi nilipo elekea na ni kitu gani ambacho kilinipata hadi nikaondoka kabla ya mechi kuanza.

“Umefanikiwa?”

“Ndio mwalimu yule pale na wazazi wake”

Nilizungumza huku nikimuonyesha alipo Camila na wazazi wake.

“Sawa anza kupasha”

Nikaanza kukimbia kimbia pembezoni mwa uwanja na kuwafanya mashabiki wa darasa langu kuanza kushangilia, wachezaji wezangu walipo ndani ya uwanja walipo niona nao wakaanza kupata hamasa ya kucheza kwa juhudi. Nikawatazama wakwe zangu, nao nikawaona wakiwa wamkini sana wakifwatilia mpira huu huku wakiwa wamekaa kwenye jukwaa maalumu la wageni rasmi, kocha akaniita.

“Kiungo kimepwaya, na hata ngome yao ni ngumu sana kuipita yule beki niliye kuonyesha ana cheza namba tano, hakikisha kwamba unakuwa naye makini”

“Sawa mwalimu, zimebaki dakika ngapi kabla ya kipindi cha kwanza kuisha?”

“Dakika kumi”

“Sawa”

Yakafanyika mabadiliko, akatoka mshambuliaji mmoja kisha nikaingizwa mimi. Uwanja mzima ukarindima kwa shangwe, kila mtu akafurahi uwepo wangu uwanjani. Hofu ikaanza kuwapata wachezaji wa darasa la sita, mimi na rafiki yangu Rafael ambaye huwa tunaendana sana kwenye swala la uchezaji na ushambuliaji, tukaanza kupeleka mashambulizi ya kasi sana kwa darasa la sita. Ndani ya dakika nne, Rafael akafanikiwa kufunga goli la kwanza huku pasi ya goli hilo ikitokea kwangu. Nikamuona jinsi Camila anavyo shangili huku akinipungia mkono.

“Tunaweza kurudisha?”

Niliwahimiza wachazaji wezangu huku nikipotea kitambaa cha kuongoza timu kutoka kwa golikipa. Mpira ukaanza kwa kasi ya ajabu huku wachezaji wezangu wakijitahidi kwa hali mali kuhakikisha kwamba tunakomboa hili goli moja lililo sali, nikafanikiwa kupata mpira huku mbele yangu kukiwa kumebakia mabeki wawili, mmoja ndio yule ambaye kocha aliniambia niwe naye makini. Mabeki hawa wawili wakanifwata kwa kasi sana, nikiwa katika harakati za kuwapita, kutokana na uwefu wa vimo vyao, nikahisi kisi kitu kizito kikinipiga kichwani mwangu na mzima mzima nikaanguka chini na giza nene taratibu likaanza kupoteza nuru ninayo iona kwenye mboni za macho yangu na baada ya sekunde kadhaa nikapoteza kumbukumbu.



Vilio vya sauti ya Camila, vikaanza kuchukua nafasi kwenye ufahamu wangu wa akili, nikajaribu kuyafumbua macho yangu, ila sikuweza kuwaona watu vizuri, ila niliweza kumuona Camila pamoja na watu walio valia makoti meupe.

“Inabidi usubirie hapa, sisi tunaingia ndani”

Niliisikia sauti ya kiume, kisha nikaona muelekeo wa kitanda nilicho lalia ukibadilika, nikawaona madaktri wakisaidia kuniwe juu ya kitanda kingine, taa kubwa zilizo washwa, zikazidi kuyafanya macho yangu kushindwa kabisa kuweza kuona na kungundua ni kitu gani ambacho kinaendelea. Hali ya kusikia sauti za watu nayo ikaanza kupungua na mwishowe sikuweza kusikia kitu cha aina yoyote.

***

Nikafumbua macho yangu na kumuona Ethan rafiki yangu akiwa amesimama pembeni ya kitanda nilicho kilalia.

“Karibu tena duniani”

“Mbona upo hapa?”

Nilizungumza huku nikiandelea kutazama mazingira ya eneo hili.

“Nimekuja kukujulia hali kwani ni vibaya?”

“Hapaana, sasa hivi ni saa ngapi?”

“Saa nane usiku”

“Duu”

Nilizungumza huku nikihisi maumivu makali sana ya kichwa changu, nikajishika na kujikuta kichwa kikiwa kimezungushiwa bandeji kubwa.

“Kwa nini hukunisaidia, nilipo kuwa nina pata hii ajali?”

“Nilikuwa mbali”

Mlango ukafunguliwa na akaingia nesi mmoja, akanisogelea hapa kitandani pasipo kumuona Ethan.

“Unajisikiaje Ethan?”

“Kidogo nafuu japo kichwa kina nigonga sana”

“Pole sana mtoto mzuri utapona sawa”

“Sawa”

“Ugua pole na asubuhi daktari atakuja kukuona”

“Sawa nesi”

Nesi huyu akatoka na kuniacha na Ethan.

“Siku nyingine unatakiwa kuwa makini sana kwenye mpira”

“Ila uliniambia umenipa nguvi, la sijaona matumizi yake?”

“Kwa sasa nimekuambia kwamba muda wake bado. Ukifika wewe mwenyewe utaweza kuona ni kiasi gani cha nguvu na mamlaka ambayo unayo ila kwa sasa usiwe na haraka”

“Sawa”

Tukazungumza mambo mengi sana na Ethan, hadi majira ya asubuhi, akaondoka na kuniahidi kwamba atarudi mchana. Madaktari wakaingia ndani humu na kunijulia hali, wakanichoma sindano ya kupunguza maumivu na kunipatia vidonge. Nikawajaribu kuwadadisi ili niweze kutambu ni tatizo gani ambalo linanisumbua, ila hapakuwa na hata mmoja aliye weza kuniweka wazi na wakaniomba niweze kumsubiria wazazi wangu.

Ilipo timu saa moja kamili bibi Jane Klopp na mume wake mzee Klopp wakafika hospigtalini hapa.

“Unaendeleaje?”

Mzee Klopp aliniuliza huku akionekana kuwa na wasiwasi nami.

“Naendelea vizuri tu baba”

“Pole sana mwanangu”

“Asante baba”

“Madaktari wamekuambia kwamba una sumbuliwa na nini?”

Bi Jane Klopp aliniuliza kwa sauti ya upole na iliyo jaa masikitiko.

“Hawajanieleza, jana niligongana na mchezaji mwenzangu na nikapoteza fahamu”

“Pole sana”

Daktari akaingia na akamuomba mzee waweze kwenda kuzungumza ofisini na hapa chumbani nikabaki na bibi Jane Klopp.

“Ethan kuna tetesi nimezisikia ila nahitaji kuzi dhibitisha kwako”

“Tetesi zipi?”

“Nilisikia kwamba jana mjukuu wa raisi alitaka kujiua na wewe ukamuokoa na yote ni kutokana ana kupenda?”

Nikastuka hadi bibi Jane Klopp akalitambua hilo.

“Sizungumzi hivyo kwa ajili ya kukuhukumu, hapana jambo la upendo ni la kila mmoja, si mkubwa na wala si mtoto. Wewe kupendwa si jambo baya”

“Ni kweli mama Camila alini……”

Kabla ya kuzungumza tukashuhudia mlango ukifunguliwa, akaingia mama Camila pamoja na mume wake. Bibi Jane Klopp akanyanyuka kitandanina kuwapokea kwa heshima sana, nikawasalimia wazazi wa Camila huku mama Camila akinikabidhi uwa zuri kubwa.

“Unaendeleaje?”

“Ninaendelea kidogo nafuu”

“Pole sana, jana kwa kweli tulipata mstuko mkubwa sana baada ya kuona ajali ile uwanjani”

“Naendelea vizuri”

“Jane huyu ni kijana wako?”

“Ndio nikijana wangu”

“Nina furaha sana kusika hivyo kwa kweli. Mzee Klopp akaingia ndani humu huku akiwa ameongozana na daktari. Wakasalimiana na wazazi wa Camila, daktari akanieleza kwamba nimepata ruhusa ya kuelekea nyumbani na atakuwa akija nyumbani kunitembelea.

“Kwa hiyo sinto rudi shule?”

“Hapana, inabidi upate muda mzuri wa kupumzika”

“Ila dokta hali yake si inaendelea vizuri”

“Yaa itakuwa vizuri maelekezo yote nimempatia mzee hapa”

“Sawa”

Taratibu za kutoka hapa hospitalini zikamalizika, tukaagana na wazazi wa Camila huku wakiniahidi kwamba jioni ya leo mtoto wao atakuja nyumbani kwetu kuniona. Tukaingia kwenye gari na safari ya kuelekea nyumbani ikaanza.

“Ethan kupata ajali kama hizi kwenye mpira ni jambo la kawaida sana, isije ikatoke ukachukia mpira”

Mzee Klopp alizungmza huku akinitazama usoni mwangu.

“Siwezi baba”

“Hivi unajua mzee wako naye zamani alikuwa ni mchezaji mzuri”

“Wee”

“Yaa alikuwa anachezea Dotmund”

“Tukifika nyumbani nitakuonyesha picha zangu kipindi nilipo kuwa mchezaji”

“Sawa”

Tukafika nyumbani, nikamkuta dada Mery sebleni, akanipokea kwa furaha tofauti na siku zote. Tukapata chakula cha mchana huku dada Mery akiniomba msamaha kwa yale yote ambayo yaliweza kutokea kwa siku za hapo nyuma. Furaha na amani ikarudi katikati yetu. Mzee Klopp akaanza kunitembeza kwenye chumba chake ambacho kina picha na vifaa vyake vya zamani akiwa mchezaji toka alipo kuwa mtoto hadi umri ambao alimua kustafu mpira.

“Unataka kuniambia huyu alikuwa ni wewe?”

Nilizungumza huku nikiwa nimeshika picha moja, ikimuonyesha mzee Klopp akiwa kijana mdogo sana.

“Yaa ni mimi, nilikuwa ninacheza namba kama unayo cheza wewe, ila kabla ya hapo nilikuwa nacheza kama beki, ila nilipo jigundua kwamba nina uwezo wa kufunga, kupiga chenga na kumiliki mpira kwa muda mrefu basi niliweza kujibadilisha mfumo wangu wa uchezaji na kuwa mfungaji, hadi nina stafu ndani ya kablu ya Dodtmud nimefunga magoli mia tatu na tano na historia yangu haijavunjwa na mtu wa aina yoyote hadi sasa hivi”

“Duuu, ina maana huku hama timu?”

“Yaa nilianza kwenye timu hiyo nikiwa mtoto na hadi nikastafu. Nikawa kocha wa timu hiyo kwa miaka saba baada ya hapo niliamua kustafu na kuendelea na mambo yangu ya biashara”

“Safi sana baba”

Mzee Klopp akanikabidhi tisheti yake moja”

“Hii tisheti itunze ukikua utaivaa. Hakikisha kwamba jina la baba yako huliangushi chini”

“Nakuahidi nitacheza mpira kwa jihudi zangu zote”

“Nafurahi kusika hivyo”

Tukaendelea kutembea maeneo mbali ya jumba hili, hadi jioni, tukarudi nyumbani na tukamkuta Camila akiwa na mama yake pamoja na bibi Jane Klopp. Camila alipo niona hakujali kuna watu wazima, alicho kifanya ni kunikimbilia na kunikumbatia kwa nguvu. Mzee Klopp akanikonyeza kisha akaondoka.

“Unaendeleaje mpenzi wangu?”

“Kidogo ninajisikia nafuu”

“Vipi madaktari wamesema kwamba umeumia sana?”

“Hapana, nahisi ni mtikisiko tu”

“Kichwa hakiumi?”

“Hakiumi nilikunywa dawa asubuhi”

“Pole mwanya, yaani leo siku nzima nimeshindwa kusoma. Nilipoteza furaha kabisa mpenzi wangu”

Camila alizungumza huku tukielekea kwenye moja ya bustan yenye majani mazuri.

“Usijali vipi timu yetu ilifanikiwa kusonga mbele?”

Camila akatingisha kichwa kwa masikitiko akimaanisha kwamba timu yetu iliweza kufungwa na kutolewa kwenye mashindano. Habari hii kusema kweli ikanisononesha moyo wangu.

“Tulifungwa goli ngapi?”

“Tano mbili”

“Mmmmm”

“Yaani baada ya kuanguka wewe, timu nzima nasikia ilichanganyikiwa, wachezaji wakapoteana uwanjani, yaani nasikia kipindi cha pili kilikuwa kibaya sana kwetu”

“Duu”

“Yaani inaonyesha dhairi wewe ndio roho ya timu”

“Mungu akijalia mwakani tutaendelea”

“Ucheze vizuri ili usije ukapata ajali kama hii”

“Usijali mpenzi wangu”

Tukaa chini pembezoni mwa bwawa lililopo katikati ya bustani hii, taratibu Camila akanilalia begani mwangu na akaanza kuimba nyimbo moja nzuri ambayo kusema kweli ikaniburudisha moyoni mwangu.

***

Kadri siku zilivyo zidi kusonga mbele ndivyo jinsi penzi langu mimi na Camila lilizidi kupamba moto, si shule tu, hata mitaani penzi letu ziliweza kuzungumziwa na watu wengi. Wapo baadhi waliponda mahusiano yetu wakidai sisi bado ni watoto wadogo sana na wapo ambao waliweza kutupongeza na kutuombea mema kwenye mahusiano yetu. Muhula wa mwisho, Camila akashika nafasi ya kwanza darasani huku mimi nikishika nafasi ya kumi jambo ambalo kidogo liliniuma. Sikusita kumpongeza mpenzi wangu kwa juhudi alizo ifanya.

“Tukiingia darasa la pili hakikisha kwamba unashindana nami kwenye masomo sawa”

“Sawa mpenzi wangu”

“Nataka siku na wewe ushike nafasi ya kwanza ili watu waweze kujua kwamba hata nyinyi watu weusi munaweza kuwazidi wazungu akili na kinato tutofautisha hapa ni rangi za miili yetu tu”

Maneno ya Camila kusema kweli yakanihimiza sana na kunipa moyo na hamasa ya kupania nikirudi mwakani ni lazima nishindana naye kwenye masomo yetu.

“Nashukuru mpenzi wangu kusikia hivyo”

“Sawa kesho nitakuja kwenu tushinde siku nzima”

“Sawa”

Camila akaingia kwenye gari lililo kuja kumchukua, kisha na mimi nikaingia kwenye gari latu na safari ya kurudi nyumbani ikaanza. Katika kipindi chote cha likizo mzee Klopp alinifundisha mbinu nyingi sana katika upande wa uchezaji wa mpira.

“Kesho tutaelekea kwenye kituo cha timu ya Dotmud kwa ajiki ya kuanza mazoezi na watoto wezako. Ukifanya vizuri utasajiliwa haraka sana, nina imani hoto niangusha”

“Siwezi kukuangusha baba”

Nilizungumza huku nikiwa nimejawa na furaha sana moyoni mwangu kwa maana hii ni habari nzuri kwangu na kipaji changu kwa ujumla.Kama alivyo niahidi mzee Klopp siku iliyo fwata alfajiri na mapema tukaingia kwenye gari na kuelekea kwenye makao makuu ya timu hiyo. Wachezaji wakubwa na makocha wote wakaonekana kumpa heshima kubwa sana.

“Ethan”

“Ndio baba”

“Ukijitahidi kwenye maisha yako, hii ndio heshima ambayo utaipata, hapa uwanjani nimeacha heshima yangu na kuna sanamu lililo chongeshwa na kufanana na mimi, lipo nje ya uwanja pale, nitakuonyesha tukitoka”

“Lina maanisha nini hilo sanamu?”

“Ni heshima, hakikisha kwamba una vunja rekodi yangu na una endeleza uhodari wa jina langu”

“Sawa baba”

Tukaingia kwenye moja ya ofisi, na kuwakuta wazee wawili ambao wote wakamsalimia mzee Klopp kwa heshima, nikawasalimia wazee hawa kwa heshima.

“Nimeleta mkombozi mpya wa timu, sasa jukumu liwe kwenu sasa kumuendeleza”

“Anaweza kweli?”

“Mimi sio muongeaji sana, si vijana wapo uwanjani, twendeni tukamjaribu”

Tukaondoka ofisi humu na kuelekea kwenye viwanja vya mazoezi, nikakuta timu ya watu wakubwa wakicheza katika kiwanja chao, huku timu ya vijana wenye umri wa kati wakicheza kwenye uwanja wao huku kiwanja cha tatu wakicheza wachezaji wenye umri kama wangu wa miaka saba hivi. Nikawatazama watoto hao, nikaona wanacheza kawaida.

“Baba ninaweza kujiunga na vijana hao wakubwa wakubwa?”

Kauli yangu ikawafanya wazee hawa kunitazama kwa mshangao.

“Kijana ana omba fursa nawasikiliza nyinyi”

“Twende tukakuombee kwa kocha wa vijana”

Tukafika kwa kocha wa vijana, kocha alipo elezwa kwamba nina hitaji kucheza kwenye timu yake, naye akaonekana kushangaa kidogo.

“Ila anapaswa akaanze kule chini”

“Nina omba nikishindwa basi nina toka nitaenda kucheza kule chini”

Nilizungumza kwa kujiamini. Kocha kanitazmaa kwa mshangao, kisha kwa ishara akaniomba nivue suruali yangu ili niweze kupewa jezi ya mazoezi. Kutokana nilisha jiandaa kwenye swala la viatu, sikuwa na haja ya kuvua viatu. Nikavaa bukta inayo nitosha, pamoja na tisheti. Mwalimu akagawa vikosi viwili huku wezangu ambao nimechaguliwa nao kwenye kikosi ninacho chezea, walianza kulalamika kwamba mimi ni mdogo sana na wengine wakaenda mbali sana na kudai kwamba ninatakiwa kujiunga na watoto wezangu. Kocha msaidizi, akaanzisha mechi hii. Wachezaji wezangu wakawa wazito sana katika kunipatia mipira huku wengi wao wakionekana kuto kuni amini. Ikanilazimu nicheze kwa kujitegemea, nikaanza kukaba, nikafanikiwa kupata mpira, kasi na nguvu alizo barikiwa zikaniwezesha kuweza kuwapiga chenga wachezaji wa kiosic ha pili, na nilipo fika karibu na goli, nikapiga shuti moja zito, kwa bahati mbaya likagonga mwamba hadi mwamba ukatingishika na kumfanya kipa kunikodolea macho. Wachezaji wote wakabaki wakishangaa kwa uwezo wangu nilio uonyesha, nikamtazama mzee Klopp nikamuona akiniyooshea dole gumba.

Tukaendelea kucheza mpira, wachezaji wa kikosi changu wakaanza kuniamini, na kunipatia pasi, katika mashuti sita niliyo piga golini, manne nikafunga na mawili yakagonga mwamba. Wachezaji wa timu kubwa, nikaanza kuwaona mmoja baada ya mwengine akijongea kwenye kiwanja chetu kutazama uwezo wangu.

Kitu kingine nilicho barikiwa, ninaweza kupiga chenga kiasi kwamba wachezaji wengine wanaogopa kunikabili kwani ninaweza kuwadhalilisha chenga zangu. Hadi mapumziko, nimefunga goli tano.

“Ethan”

Mzee Klopp aliniita, nikatoka uwanjani na kusimama mbele yao.

“Inatosha mwanangu, sasa wazee munaweza kuzungumza biashara hapa hapa, nimewaletea Klopp Jr ambaye atarudisha heshima ya timu na vikombe sasa vitaanza kurudi kwenye club yetu siku si nyingi. Wazee hawa wakabaki midomo wazi huku kila mmoja akiwa hana usemi.

“Huyu kijana ni nani?”

Kocha wa timu kubwa aliuliza huku akinitazama.

“Ninaitwa Ethan Klopp”

“Klopp ni mwanao?”

“Ndio”

“Nimeona kitu kikubwa ndani yake, kitu ambacho kusema kweli sinto hitaji kukipoteza”

“Bora na wewe umeona, wezako hapa wana shangaa. Sasa tuzungumzeni biashara, munamsajili au niondoke na kijana wangu akawe zao la timu nyingine”

“Weee tukikataa nahisi tutakuwa wendawazimu, mtu unaona kwamba tumeletewa Mess alafu tumkatae. Klopp mimi nipo tayari mkusajili”

“Kiwango cha chini ni paund milioni kumi kama munapesa tuingie mezani, ila kama hamuna kesho nina panda naye ndege ninaelekea naye Hispani na huko munafahamu kuna mapapa wakubwa R. Madrid na Bacelona”

“Klopp kumbuka wewe hapa una heshima, usitufanyie hivyo bwana?”

“Nina heshima, ila huku anakwenda kuvunja rekodi na heshima yangu, siwezi kumuachia bure kwa maana ni zao langu hili na si lenu”

Mzee Klopp aliendelea kushikilia msimamo wake wa kuhitaji kuniuza katika timu hii jambo ambalo ni jema sana kwenye maisha yangu ya mpira nikiwa bado ni kijana mdogo wa miaka saba.



Viongozi hawa wa hii timu ya Dotmund wakaa kimya huku wakitutazama mimi na mzee Klopp.

“Basi tutalizungumza mzee Klopp”

“Sawa, munamruhusu kijana wangu akaendelee na mazoezi yenu au tuondoke?”

“Muache tu aendelee na mazoezi hakuna tabu”

Kocha wa timu ya vijana alizungumza huku akiwa na tabasamu sana. Nikarudi uwanjani na nikaendelea kuonyesha uwezo wangu mara mbili hata na mara ya kwanza nilipo kuwa nikicheza kwa maana nimesikia kiwango cha pesa kilicho tajwa kwa ajili ya mimi kununuliwa. Hadi tunamaliza mazoezi tayari nimefunga goli nane peke yangu huku nikitoa mchango wa goli mbili. Kila mchezaji akatokea kunipenda huku wachezaji wengine wakubwa wakiomba kupiga nami picha. Hapa ndipo nilipoa anza kuigundua nguvu niliyo nayo kwa maana wachezaji vijana wao ndio huwaomba wachezaji wakubwa kupiga nao picha, ila kwangu imekuwa tofauti ya hivyo. Nikapiga picha na wachezaji karibia wote huku wengine wakinionyesha video za magoli ambayo nimeyafunga.

“Hei Ethan”

Mchezaji mmoja mkubwa aliniita na akasogea na mimi pembeni.

“Unajua nini juu ya hii Club?”

“Hii Club alicheza baba yangu mzee Klopp yule pale”

“Hilo ndio unalo lijua?”

“Ndio”

“Una kipaji kikubwa sana, tena sana mdogo wangu. Ninacho kushauri usikubali kusajiliwa katika timu hii, ligi yetu ya hapa Ujerumani bado haijapata nguvu kama ligi ya nchini Uingereza na Hispania. Mshauri baba yako akupeleke ukafanye tena majaribio kwenye timu kubwa kama Liverpool, Man City, Man United, Arsenal, Madrid au Bacelona. Nakuhakikishia baada ya miaka mitano mbeleni utakuwa bilionea sawa”

“Sawa kaka”

“Liweke hilo akilini na usimuambie mtu mwengine zaidi ya baba yako”

“Sawa”

Mchezaji huyu akanikunjia ngumi mkono wake wa kulia, nami nikakunja nguni na kuzigonganisha, kisha kaniruhusu kuelekea kwa baba yangu mzee Klopp.

“Ethan”

“Ndio baba”

“Una kipaji sana leo umenitoa kifua mbele kwenye hii club”

“Asante sana baba”

“Mazoezi mengi, kujituma na heshima hilo ndio jambo kubwa na la muhimu sana kwenye mpira wa miguu. Zingatia hayo pasipo kumuangalia mtu wala pasipo kupenda umaarufu. Si unaona watu wanakufwata wenyewe?”

“Ndio baba”

“Ukijitahidi katika hayo, kila jambo litakwenda kufanikiwa kwa upande wako sawa”

“Sawa baba”

“Sanamu ambayo nilikuwa ninaizungumzia muda ule ndio hii hapa”

Mzee Klopp akanionyesha sanamu moja kubwa sana inayo fanana na yeye, ila hii inamuonyesha enzi zake akiwa mchezaji.

“Aliye ichonga hii sanamu ni nani?”

“Ni mmoja anaitwa Karius, ila kwa sasa ni marehemu, yeye ndio aliitengeneza hii sanamu na kuiuza kwenye hii Club, ni heshima kubwa sana kwangu kuwekwa kama hivi. Naamini kwamba na wewe siku moja ukiwa mtu mwenye makamu kama yangu basi nawe utawekwa kama hivi”

“Nitahakikisha baba, sanamu langu linakuwa kubwaaaa kupiga hata hili la kwako”

“Hahaaa hilo ndio jambo ninalo hitaji kulisikia nahitaji uvunje rekodi ya mchezaji mmoja hapa duniani ambaye hadi sasa hivi haijawahi kuvunjwa”

“Mchezaji gani baba?”

“Anaitwa Edson Arantes do Nascimento”

“Heee ndio nani huyo!?”

Niliuliza huku nikiwa nimejawa na mshangao mkubwa sana.

“Jina lake maarufu anaitwa Pele. Ni mchezaji maarufu duniani kwa kipindi chote toka karne ya ishirini hadi sasa. Hakuna mchezaji ambaye aliweza kuivunja rekodi yake ya magoli”

“Kwani amefunga magoli mangapi?”

“Magoli elfu moja na sabini na nne”

“Mmmmm”

“Ndio kwa umri wako unaweza kuyafikia. Hakikisha kwamba una yafikia na kuyapita”

“Baba ila magoli elfu ni mengi sana”

“Nalitambua ila kila mechi ukiweka wastani wa kufunga magoli matatu. Ukicheza mechi mia tatu hamsini na nane utakuwa umeyafikisha hayo magoli.”

“Duu”

“Yaa unajua mpira ni kama familia. Jinsi unavyo panga idadi ya watoto wako unao wataka kuzaa na kuwalea ndivyo jinsi utakavyo panga jinsi ya kufunga. Hakikisha kwamba kila unapo ingia uwanjani unaweka nia na kunuwia kwamba ni magoli mangapi ambayo una yahitaji, kufunga kwa siku hiyo. Endapo una pata nafasi funga kama leo ulivyo funga magoli nane sawa”

“Sawa baba”

“Nakuambia mambo haya, sikuwahi kumuambia mchezaji wangu yoyote hata pale nilipo kuwa kocha. Fanyia kazi haya maneno yangu, utaona jinsi dunia itakavyo kuheshimu sawa”

“Sawa baba”

Mzee Klopp akaendelea kunitembeza katika maeneo tofauti tofauti ya uwanja huu mkubwa wa mpira. Baada ya kumaliza matembezi haya, akanipeleka kwenye mabafu nikaoga na kuvaa nguo zangu. Safari ya kurudi nyumbani ikaanza taratibu.

“Baba nina weza kukuuliza sawali?”

“Ndio unaweza kuwa huru”

“Hivi ni club gani ambayo kwa mtazamo wako unaweza ona nitafanikiwa kufikisha kiwango hicho cha magoli hapa duniani?”

Mzee Klopp akaka kimya kidogo huku akionekana kulifikiria swali nililo muuliza.

“Club kubwa?”

“Ndio baba”

“Kusema ukweli, ukicheza nje ya hapa Ujerumani, hilo linawezekana kwa maana ligi ya huku, moja ni ngumu sana, pili ina wendawazimu wengi sana ambao, wao hawato ona huruma kukuvunja wewe miguu na wao wakapewa kadi nyekundu zitakazo waweka nje ya uwanja kwa baadhi ya mechi tu kisha wao wakarudi, ila wewe utaendelea kuuguza majeraha”

Mzee Klopp alizungumza kwa upole sana na umakini wa hali ya juu.

“Ligi ya Uhispania, kule kwa sasa kuna wafalme wawili tu wanao onekana kuliko wachezaji wengine. Wao ni Ronaldo na Messi. Hadi ukiwa mkubwa wewe hawa watu watakuwa wamesha stafu kucheza, ila kwa ligi ya Hispani siipendi sana japo ina pesa nyingi”

“Je ligi ya Uingereza?”

“Uingereza ligi yake haieleweki, haina mbabe, timu inaweza kupanda daraja na ikachukua ubingwa. Niligi yenye ushindani mkubwa sana naamini kwa wewe itakufaa kama kweli utakuwa unaipenda sana ligi hiyo”

“Ninaweza kukuomba kitu?”

“Ndio niombe mwanangu”

“Unaonaje ukanipeleka Uingereza nikafanya mazoezi japo kwenye timu moja wapo kubwa ili uangalie wapi wataweka kiasi kikubwa waninunue?”

“Hilo ni wazo moja zuri sana. Hakika wewe una akili sana, sikukaa na kulifikiria hilo, moyo wangu na mapenzi yangu niliyaelekezea Dotmund. Ila kutokana kwa sasa mpira ni biashara na fursa ya kutengeneza historia yako binafsi nitakupelekea jijini Liverpool ukajiunge na majogoo hao wa London kwa kufana mazoezi, ukipita hakuna shaka kwa maana utakuwa upo katika timu salama”

“Sawa baba”

Tukafika nyumbani na kumkuta Merry na mama wakiwa na furaha sana ambayo kwa haraka haraka wanaonekana kuna jambo wameliona.

“Yaani Ethan kwenda tu huko leo, ona ulivyo zagaa kwenye mitando ya kijamii, tazama jinsi wachezaji wakubwa walivyo weka picha zako Instergram”

Mery alizungumza huku akionionyesha picha hizo kwenye simu yake.

“Tena honey kuna habari nyingine nzuri sana”

Bibi Jane Klopp alizungumza.

“Kuna simu mbili moja imetoka nchini Hispania, raisi wa Real Madrid anahitaji kuzungumza na wewe na simu nyingine imetoka Uingereza, tajiri wa Chelsea Roman Abramovich wote wanahitaji kuzungumza juu ya Ethan”

Mzee Klopp akanitazama huku akiwa ametabasamu kwa furaha sana.

“Tena wamesema ikiwezekana wakutumie hata private jet uende na Ethan katika hizo timu”

Nikamuona mzee Klopp akiwa kama amewehuka kwa furaha, mara azunguke huku mara achukue simu ya hapa sebleni mara airudishe.

“Wametumia simu ile ya nyumbani”

“Niletee”

Bibi Jane Klopp akaanza kutembea kuelekea ndani huku akiwa katika mwendo wa haraka haraka. Kusema kweli furaha imenijaa sana moyoni mwangu. Bibi Klopp alirudi hapa sebleni haraka haraka huku simu hiyo ikiwa inaita.

“Ni namba kutoka Uingereza”

“Uingereza?”

“Ndio mume wangu?”

Mzee Klopp akaichukua simu hiyo, akaipokea na kuiweka sikioni mwake.

“Ndio”

“Sawa”

“Tutakuja”

“Basi nitawapa maelezo yapi ya kufwata”

“Sawa sawa”

“Haya”

Mzee Klopp akakata simu na kuanza kushangilia seble nzima hadi sote tukaanza kumcheka.

“Ethan ndoto yako imekuwa kweli”

Mzee Klopp alizungumza huku akininyanyua na kunikumbatia.

“Unakwenda Liverpool”

“Kweli baba”

“Niamini, acha kwanza tukazungumze na timu ya Liverpool”

Mzee Klopp aliendela kuzungumza huku akiwa amenibeba.

“Muweka mwenzako chini usije ukamuangusha”

“Siwezi kumuangusha kabisa, sasa inabidi muanze kumuandalia nguo, leo nina panga utaratibu wa ndege yao wanayo ituma kisha kesho tunaanza safari kuelekea Uingereza sawa”

“Sawa baba”

Niliitikia nikiwa na furaha sana. Mery akaniita na kuninong’oneza.

“Usiondoke pasipo kumuambia chochote Camila”

“Ninaweza kuwasiliana naye kupitia simu yako?”

“Ndio”

Mery akanipatia simu yake na nikakimbilia chumbani kwangu. Nikampigia Camila kupitia simu ya mama yake, akapokea, nikamsalimia mama yake na kwa bahati nzuri hakuwa mbali na Camila.

“Ethan mbona leo una furaha sana?”

“Nimeitwa katika kikosi cha watoto cha timu ya Liverpool jijini London”

“Ethan acha utani?”

“Haki ya Mungu vile baba ametoka kupigiwa simu sasa hivi”

Camila hakunijibu kitu chochote zaidi ya kukaa kimya.

“Halooo”

“Ethan?”

“Ndio mpenzi wangu”

“Huto niacha kweli ukienda huko?”

Camila alizungumza kwa unyonge sana hadi furaha yangu ikaanza kunipotea.

“Mpenzi wangu, siwezi kufanya chochote kibaya juu ya penzi letu”

“Ethan najua ni jinsi gani ninavyo kupenda, ukienda huko ni lazima wahitaji ubaki huko huko, na mimi sitaki mpenzi wangu iwe hivyo”

“Nakuapia Camila kwa jina la Mungu, siwezi kukusaliti. Najua unapenda kuniona ninafanikisha ndoto zangu, nakuomba unipe nafasi yenye baraka niweze kufanikisha ndoto zangu mpenzi wangu sawa”

“Sawa Ethan, ukienda kesho munarudi lini?”

“Sijajua kwa maana ninakwenda kufanyiwa majaribio ya kwanza, nikiwanikiwa basi tutajua ni lini nitatakiwa kurudi tena Uingereza”

“Ila Ethan kuwa makini, sasa hivi utanipoteza kabisa duniani kwa maana nina kupenda sana”

“Siwezi kukupoteza wewe ni wangu tu”

“Kweli?”

“Ndio mpenzi wangu”

“Sawa tutazungumza usiku sasa hivi tunajiandaa na mama tunataka kwenda mjini kwenye maduka”

“Poa nina kupenda Camila”

“Ninakupenda Ethana wangu mwaaaa”

“Asante mpenzi wangu”

Camila akaka simu na kunifanya nijawe na furaha sana moyoni mwangu, ndoto za kuwa mchezaji mkubwa duniana zinaanza kutimia taratibu.

‘Ethan”

Niliisikia sauti ya Ethan mwenzangu, ikiniita nyuma yangu ambaye uhalisia wake ni jini.

“Shitii umenistua sana”

‘Nisikilize sina muda mwingi sana. Kesho usiende hiyo safari kwa maana mukifika nchini Uingereza mmoja wenu kati ya baba yako au wewe atapigwa risasi na kufa hivyo musiendeee”

Maneno ya Ethan yakanistua sana moyo wangu, hakuhitaji hata nimuulize swali, akapotea mbele ya upeo wa macho yangu na kunifanya niwe katika wakati mgumu sana ulio iyeyusha furaya yangu mithili ya barafu katika jua kali.



“Ethan kwa nini tusiende”

“Nimekuambia kwamba sina muda mwingi, hakikisha kwamba safari hii haifanikiwi sawa”

Ethan mara baada ya kuzungumza hivyo akapotea mbele ya uwepo wangu wa macho. Wasiwasi mwingi ukazidi kunitawala, hamu ya kwenda Uingeraza yote ikaniishia. Nikajikuta nikikaa chini na machozi yakianza kunimwagika.

‘Ethan niambie basi kama ulicho nieleza ni uongo’

Nilizungumza huku machozi yakinimwagika usoni mwangu. Nikiwa katikati ya hali ya huzuni, mlango ukagongwa na nikasikia sauti ya Mery akiniita.

“Ethan umesha maliza?”

“Ndio dada ninakuja”

Nilizungumza huku nikianza kujifuta machozi yangu usoni. Nikaendelea kujifuta hadi nikamaliza. Nikanyanyuka kwa haraka na kufungua mlango. Mery akanitazama usoni mwangu huku macho yake akionekana kama mtu mwenye mashaka juu yangu.

“Ulikuwa una lia?”

Mery aliniuliza huku akiwa amenikazia macho.

“Hapana nilikuwa nina omba dada, kwa maana ni batati kubwa niliyo ipata”

“Ninaweza kuingia?”

“Ndio”

Mery akaingia na kukaa kitandani kwangu nami nikaka kitandani kwangu huku nikimtazama.

“Ethan ni mambo mangapi ulisha wahi kudanganya?”

Swali la Mery likanistua kidogo

“Kivipi dada?”

“Mimi ni daktari na ninauwezo mkubwa sana wa kumgundua mtu akifanya jambo hilo nikiwa nina mtazama tu machoni mwake. Natambua kwamba haukuwa una Sali, niambie ukweli ni kitu gani ambacho kimekukosesha furaha na amani?”

Nikajifikiria kwa muda huku nikiwaza nimueleze ukweli juu ya hili nililo ambiwa na Ethan, ila kusema kweli bado ninapata kigugumizi.

“Au Camila amekukataza kwenda huko?”

“Ndio dada”

“Ohoo usijali, nitazungumza na mama yake amshawishi ili akubali muende”

“Amesema kwamba tukienda huko anahisi kuna jambo baya litatokea”

“Hahaa…ana wivu tu, hakuna kitu kibaya ambacho kitakwenda kuwapata wewe na baba sawa. Kikubwa ni wewe ujiandae kwa safari kesho na hakikisha kwamba ukifika una muwakilisha baba vizuri, sawa Ethan”

Maneno ya Mery yakazidi kuniny’ong’onyeza japo nimejaribu kupindisha ukweli, ila anaonekana haelekei kabisa katika pointi yanug ya msingi ambayo nimeimaanisha.

“Sawa dada”

“Leo nitatoka kwenda mjini, nitakuletea nguo nzuri za kuvaa kesho sawa”

“Sawa dada”

Mery akatoka ndani humu huku akiwa ameishika simu yake mkononi. Nikajilaza kitandani huku nikijaribu kufikiria safari ya kesho ambayo tayari imesha anaza kuingia kikwazo. Nikajaribu kumuita Ethan kwa mara kadhaa ila hakuweza kuitika, wala kuzungumza nami katika ufahamu wangu wa akili. Usingizi taratibu ukanipitia kwani ukichanganya na uchovu wa mazoezi na kuamka asubuhi sana na mapema, sikuwa na sababu yoyote ya kuto kuacha kulala.

**

Familia nzima ikatusindikiza hadi katika uwanja wa ndege huku tukiwa na wawakilishi wa wawili kutoka katika timu ya Liverpool. Kila mmoja wetu kusema kweli furaha imemjaa usoni mwake, kwani safari hii ni ya mafanikio na kila mtu ana amani kwamba ndio mwanzo wangu mzuri wa kuingia katika soka la kulipwa huku nikiwa na umri mdogo sana.

Tukaingia katika ndege binafsi iliyo tumwa kutoka nchini Uingereza. Tukaingia na kukaa katika siti nzuri ambazo zimewekwa katika eneo lililo tengenezwa kwa mfumo kama wa sebleni, kwani kuna Tv na friji ndogo. Nikiwa katikati ya furaha, gafla akatokae Ethan na kusimama pembeni yangu, nikawatazama watu wote wa humu ndani na sikuweza kumona hata mmoja wao aliye weza kustuka kutokana na uwepo wa Ethan katika eneo hili.

‘Mbona umekaidi maneno yangu?’

Ethan alizungumza kwa sauti nzito ambayo kwa kipindi cha awali alipo kuwa akizungumza nami ndio alikuwa akiitumia.

‘Etha…..’

‘Hivi hujui kwamba nina kulinda eheee, nikikuambia kwamba usifanye kitu kwa nini hunielewi au unajiona kwamba wewe una uwezo mkubwa kuliko mimi si ndio?’

Ethan aliendelea kufoka kwa hasira. Kusema kweli leo ndio nimeweza kumuona jini huyu akifoka kwa fujo na uzuri wake wote ukatoweka. Mwili mzima ukaanza kunitetemeka.

‘Ethan nilishindwa kumshawishi baba na tayari alisha fanya mawasiliano na hawa watu ndio maana leo hii tupo humu ndani ya ndege’

Ethan akamtazama mzee Klopp anaye cheka na kururahi huku simu yake akiwa ameiweka sikioni mwake.

‘Ethan rafiki yangu nakuomba ubadilishe mambo mabaya yatakayo tokea huko mbeleni, tafadhali ninakuomba sana.’

Ethan hakuzungumza chochote zaidi ya kuniangalia kwa mcho ya hasira. Akapotea kwenye uwepo wa macho yangu na kunifanya nizidi kuogopa, nikashusha pumzi nyingi sana huku nikimtazama mzee Klopp anaye zungumza na marafiki zake. Nikatamani kuzungumza jambo ila ndege tayari imesha anza kutembea. Ndege ikaanza kupaa angani huku nikishuhudia tukiiacha ardhi ya nchini Ujerumani taratibu.

“Ethan sasa mwanangu unakwenda kuwa nyota wa dunia”

Mzee Klopp alizungumza kwa furaha sana.

“Asante baba”

“Ukijituma ndio siri kubwa ya mafanikio sawa”

“Sawa baba”

Ndege ikazidi kuchana mawingu. Gafl ikaanzaa kuyumba na kutufanya watu wanne yulipo katika eneo hili kuanza kupatwa na wasiwasi. Kwa haraka muwakilishi mmoja akajifunga mkanda siti yake vizuri. Hali ikazidi kuwa mbaya mara baada ya ngede kugeuka, juu chini, chini juu, nikamshuhudia kiti cha mzee Klopp kikichomoka na akagongeza kichwa chake kwenye meza ya tv na kikapasuka. Mlango wa ndege hii ukachomoka na upepe mwingi sana ukaingia ndani, muwakilishi mmoja naye akachomolewa huku akipiga makelele mengi sana na akapotelea hewani. Huyu muwakilishi wa pili naye nikamshuhudia akiangukiwa na firi miguuni mwake na ikakatia vipande vipande, friji hili linalo onekana ni zito kama shelf ya kuhifadhia zitu vya siri, likaanza kumbingiria na kunipabiza kwenye mbavu zangu na kujikuta nikitoa ukeleke mmoja mkali sana wa maumivu.

**

Nikastuka kutoka usingizi huku nikipiga kelele nyingi sana, nikaanza kujipapasa kwenye upande wangu katika mbavu ambapo friji imenibamiza ila nikajikuta nikiwa nipo salama salmin. Nikashusha pumzi nyingi sana huku macho yakiwa yamenitoka kisawa sawa.

“Ethan, Ethan”

Bibi Jane Klopp akaingia ndani humu huku akiniita jina langu, akaka pembeni ya kitanda changu huku akinitazama jinsi ninavyo mwagikwa na jasho jingi.

“Una nini?”

Bibi Jane Klopp aliniuliza huku akiwa amejawa na wasiwasi mwingi sana usoni mwake.

“Ni ndoto mbaya mama”

“Ohoo pole mwanangu”

Bibi Jane Klopp alizungumza huku akinikumbatia kwa nguvu.

“Ndoto yako ina husiana na nini?”

“Ajali mama, naogopa”

“Ajali ya nini?”

Bibi Jane Klopp alizungumza kwa wasiwasi mwingi sana huku akinitazama usoni mwangu. Nikashusha pumzi taratibu, kwa viganja vyake akaanza kunifuta jasho linalo nimwagika usoni mwangu.

“Baba yupo?”

“Ndio yupo ofisini kwake”

“Naomba nizungumze ndoto hii mbele yake”

“Sawa twende”

Bibi Jane Klopp akanisaidia kushuka kitandani, tukaelekea hadi ilipo ofisi ya mzee Klopp, tukamkuta yupo na wanaume wawili, kwa kuwatazama vizuri moyo wangu ukastuka sana, kwani ndio wanaume ambao nimewaona kweney ndoto niliyo iota muda mchache ulio pita.

“Ethan wasalimie wawakilishi kutoka katika timu ya Liverpool wamekuja na private jet yao ambayo kesho ndio tutaondoka nao”

Mapigo ya moyo yakazidi kunienda mbio mara baada ya mzee Klopp kuzungumza maneno hayo. Nikajitahidi sana kuiweka sura yangu ya furaha mbele ya watu hawa ila nikajikuta nikishindwa kabisa, kwani picha ya ajali tuliyo ipata ndotoni kila mara ina jirudia kichwani mwangu.

‘Ehee Mungu naomba unisaidie hili lisitokee’

Nilijitahidi kuzungumza kimoyo moyo huku nikiwatazama watu hawa. Nikawasalimia kwa heshima sana na wao wakaonekena kufurahishwa.

“Kijana wako ni mzuri sana, kwa hakika akiendelea kuwa hivi, timu itakuwa imepata mtu mzuri sana”

“Ni kweli, nimemkuza kwenye maadili mazuri ambayo nyinyi nyote mutaipenda tabia yake”

“Ethan mimi nina itwa John Mendez”

Muwakilishi mmoja alizungumza kwa furaha huku akinipa mkono.

“Nashukuru kukufahamu”

“Na mimi ninaitwa Lucas Leivis pia ni muwakilishi wa uongozi mzima wa timu ya Liverpool.”

“Nina shukuru sana kwa kuwafahamu”

“Tumeleta hund ya benk ya pand milioni kumi kwa ajili yako tu, hiyo itakuwa ni pesa yako ya kuanzia maisha utakapo kuwa jijini Liverpool kwa maana tumezungumza na mzee hapa na amakubali kwamba makazi yako yote kuanzia kesho yatahamia jijini Liverpool Uingereza.”

Macho yakazidi kunitoka hata bibi Jane Klopp akaonekana kustuka kidogo kwa kauli hiyo.

“Samahani munaweza kutupa nafasi nikazungumza na mume wangu?”

Bibi Jane Klopp alizungumza huku akimtazama mzee Klopp usoni mwake.

“Ohoo samani, jamani kwa furaha niliyo kuwa nayo nimejisahau kumtambulisha mke wangu. Anaitwa Jane Klopp”

“Tunashukuru kukufahamu maam”

“Nami pia nina washukuru kuwafahamu karibuni sana na mujisikie kama mupo nyumbani”

“Sawa sawa mama, kutokana tumesha maliza kuzungumza na mzee hapa, basi sisi acha twende, na hundi hii tunamkabidhi Ethan na hundi ya meneja wake ambaye ni mzee hapo tumesha mkabidhi hundi ya paundi milioni thelathin”

“Sawa asanteni baba zangu na Mungu awabariki”

Bibi Jane alizungumza kwa upole huku akiwatazama wawakilishi hawa.

“Tunashukuru mama yetu”

Wawakilisha hawa wakanyanyuka kwenye viti walivyo kuwa wamekalia, na wakaanza kutoka huku mzee Klopp akiwafwata kwa nyuma, huku kwa ishara akituomba tuweze kumsubiria anakuja. Tukaka kwenye viti walivyo kwua wamekali, bibi Jane Klopp akaichukua hundi niliyo pewa, akaisoma kwa muda kidogo kisha akaiweka mezani huku akiachia msunyo unao onyesha dhairi amekasirishwa na maamuzi ya mume wake. Baada ya muda kidogo mzee Klopp akaingia huku akiwa amejawa na furaha kubwa sana usoni mwake.

“Mke wangu Ethan amezidi kuing’aza familia yetu na jina langu sasa linazidi kwenda kukua”

“Hembu njoo ukae hapa na uniambie kwa nini umeamua kufanya maamuzi yako wewe kama wewe, ikiwa mtoto ni wa kwetu wote na hakuna jambo kubwa ambalo unalifanya bila ya kuhitaji ushauri wangu?”

Bibi Jane Klopp alizunguzma huku sura yake akiwa ameikunja kwa kweli.

“Jamani mke wangu, hili swala si lipo wazi?”

“Lipo wazi kivipi, umenitarifu hata walipo kuja hawa vijana eheee?”

“Mke wangu, tuliza basi jazba”

“Klopp siku zote za maisha yetu sikuwahi kukupinga kwa maamuzi yako yoyote ambayo ulikuwa unayafanya kama baba na mume kwenye maisha yangu. Ila kwa hili la Ethan kwenda kuishi Uingereza hapana. Mtoto bado ni mdogo, miaka nane na kiasi chote hicho cha pesa unahisi Ethan ataweza kuhimili vishawishi vya Uingereza tena katika jiji la Liverpool ambalo limejaa wendawazimu na walevi?”

Bibi Jane Klopp alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake. Furaha ya mzee Klopp yote ikaondoka usoni mwake na kujikuka akikaa kwenye kiti chake taratibu.

“Kwa nini umeingiwa na tamaa ya pesa mume wangu na kuamua kuchukua pesa za watu pasipo kusika chochote kutoka kwetu, kama ungeona mimi sifai kwenye hayo maamuzi yako, umeshindwa hata kumuuliza Ethan, kweli eheeee?”

“Mke wangu kwa hilo nina kuomba uni samehe, nakiri nimefanya kosa na sipendi kukuona unalia mbele ya mtoto. Ethan nina kuomba uweze kwenda nje kidogo nizungumze na mama yako”

“Hapana hawezi kwenda nje ana jambo muhimu anahitaji kulizungumza kwetu sisi na nilikuja naye humu ili aweze kuzungumza kile alicho kiota”

Mzee Klopp akanitazama usoni mwangu, akagundua wasiwasi mwingi sana ambao ninao.

“Eti Ethan mwanangu una wasiwasi wa kitu gani ehee?”

Mzee Klopp alizungumza kwa sauti ya upole na unyeyekevu sana huku akinitazama usoni mwangu. Nikajaribu kufungua kinywa ila nikajikuta nikishikwa na kigugumizi kwa maana sifahamu hata nianzie wapi kusimulia ndoto niliyo iota kwani watu wawakilishi hawa nilio waona kwa macho yangu ya nyama ndio hawa hawa nilio waona kwenye ndoto yangu.

“Baba”

“Naam”

“Mama”

“Bee mwanangu”

“Munanipenda na kunisikiliza kwa kile nitakacho waomba”

“Ndio mwanangu, zungumza chochote tutakupatia”

Mzee Klopp alizungumza kwa shahuku huku akitengeneza tabasamu zuri usoni mwake, akisubiri ni nini ambacho waomba.

“Kwa…..usala…ma wangu na nyinyi. Baba sitaki kwenda nchini UINGEREZA tena na pesa za watu nakuomba uzirudishe”

Mzee Klopp macho yakamtoka, akasimama kwa hasira huku mikono yake miwili akiipiga mezani kwa nguvu hadi mimi na bibi Jane Klopp tukastuka, kwani anaonekana kukasirika waziwazi kwa jambo nililo muomba.



“Umechanganyikiwa wewe?”

Mzee Klopp aliniliza kwa hasira sana huku akinikazia macho. Mwili mzima wa mzee Klopp ukaanza kubadilika na kutawaliwa na uwekundu fulani ambao toka nijuane naye sikuweza kumuona nao.

“Mume wangu, mtoto amezungumza kit…..”

Bibi Jane Klopp akaikatisha sentensi yake mara baada ya kunyooshewa kidole cha uso.

“Ni lazima uende Uingereza kesho, kama hutaki ni bora ukaondoka nyumbani kwangu sawa?”

Sikuyatarajia maneno haya ya mzee Klopp, furaha ikazidi kunitoweka na wasiwasi mwingi ukaendelea kunijaa. Machozi yakaanza kunimwagika usoni mwangu, sikuona haja ya kuendelea kukaa eneo hili, nikatoka kwa haraka na kuanza kukimbilia katika eneo ambalo lina bustani nyingi za maua.

‘Ethan nimeshindwa bwana na lolote litakalo tokea baya basi bwana’

Nilizungumza kimoyo moyo pasipo sauti yangu kusikika.

“Ethan, Ethan”

Niliisikia sauti ya bibi Jane Klopp, akafika sehemu hapa nilipo ni kunikumbatia kwa nguvu huku na yeye akilia, dhairi inaonyesha kwamba maamuzi ya mume wake hajakubaliana nayo.

“Fanya kumridhisha tu baba yako”

Bibi Jane Klopp alizungumza huku akiendelea kunikumbatia.

“Mama, nimeota tutapata ajali kwenye ndege na watu ambao nimewaona kwenye ajali hiyo ni wale watu walio agizwa kuja kutuchukua”

“Ajali?”

“Ndio mama, na sote tutakufa kifo kibaya mama, naogopa ndio maana nimekataa”

“Ohoo Mungu wangu, ila subiri baadae hasira ya baba yako itakapo tulia basi tutaweza kumueleza hili jambo kwa umakini sana sawa”

“Sawa mama”

“Ulimuaga rafiki yako?”

“Ndio maama na amenikubalia”

“Sawa ninakuomba usilie mwanangu, kila jambo litakuwa vizuri sawa”

“Hyaa mama”

“Pata hewa ngoja nikaendele kuzungumza naye na hili jambo pia nitamueleza”

“Nashukuru mama”

Bibi Jane Klopp akaondoka na kuniacha peke yangu. Haukupita mud asana Ethan akakaa pembeni yangu.

“Kwa nini muda wote nimekuita hujatokea?”

“Nilikuambia kwamba muda wangu ni mfupi sana wa kuzungumza nawe”

“Hembu niambie ni nini kinacho endelea”

“Nimesha kueleza mukivuka mipaka ya hapa Ujerumani, ni lazima mmoja wetu afariki dunia”

“Wewe huwezi kulizuia hili?”

“Mimi nina uwezo wa kumiliki kila kitu katika dunia hii, ila si pumzi ya mwanadamu. Hilo ni jamboa analo lijua Mungu yeye peke yake na sio sisi viumbe wengine kama sisi majini”

“Sasa tuna uwawa kwa ajili gani?”

“Sio kila binadamu ana mipango mizuri na mzee wako. Kuna mambo mengi sana mabaya alisha yafanya nje ya kazi yake ya mpira. Maadui zake wana muwinda na huko Uingereza kuna mambo mabaya alisha yafanya kipindi hicho na akaonywa asirudi ila kesho anakwenda, na wale walio kuwa wamemuonya wengi wao wamesha kufa, ila visasi vinaendelezwa na watoto wao ndio maana maisha yenu yatakuwepo hatarini.”

“Ninaweza kuona kinachoweza kwenda kutokea?”

“Huwezi, ila umetambua”

Nikashusha pumzi taratibu huku nikimtazama Ethan usoni mwake.

“Nini tufanye?”

“Njia ya pekee ni kumzuia mzee asiende, musitishe habari ya nyinyi kwenda Uingereza”

“Sasa kule naona ndio kuna mafanikio yangu Ethan nitafanyaje?”

“Hakuna mafanikio au ushindi pasipo sadaka, ni lazima mmoja wenu damu imwagike ili mafanikio yapatikane”

“Ethan unavyo zungumzia mmoja wetu, si usema kwamba baba atakufa tu, kuliko kunijumlisha mimi na yeye”

“Ukitembea na mwizi na wewe utakuwa ni mwizi hata kama si mwizi”

“Unataka kuniambai ni lazima mzee afe?”

“Si yeye, nimesema mmoja wenu hata wewe upo kwenye huo mkumbo”

“Sas nikifa utapata wapi rafiki mwengine?”

“Hahaaaa….wapo mbona marafiki wengine, mamilioni wa watu wana niabudu mimi ili waweze kufanikiwa”

“Weeee kama kina nani?”

“Kua kwanza kiumri, kiakili na kiumbo utaweza kuwatambua ni kina nani”

“Ethan niambie bwana?”

“Acha ubishi, tena wewe unapata nafasi ya kuonana na mimi na kuzungumza nami. Ila wezako wana isikia ile sauti yangu nzito tu na hakuna hata mmoja wenu aliye weza kuniona”

“Sawa mwaya”

“Tutaonana baadae kuna mambo ninakwenda kuyashuhullikia”

“Wapi?”

“Ethan si kila kitu unapaswa kufahamu kwa heri”

Ethan akaondoka na kuniacha nikiitazama sehemu aliyo kuwa amesimama. Nikarudi katika nyumba kubwa tunayo ishi, nikaelekea chumbani kwnagu, nikachukua moja ya begi langu la nguo, kwa kupitia dirishani, nikaona gari mbili nyeusi kutoka ikulu zikisimama katika eneo la maegesho, wakashuka wana usalama na akashuka Camila. Nikamuona bibi Jane Klopp akisalimiana na Camila, wakazungumza kidogo kisha wakaanza kuingia ndani. Nikatamani kutoka ila nikasita kidogo kwa maana kukaa kwetu sebleni hatuto pata wasaa mzuri wa kuzungumza.

Nikasikia mlango wangu ukigongwa, nikaruhusu anaye gonga kuingia ndani. Camila akafungua mlango, alipo niona kwa haraka akanikimbilia na kunikumbatia kwa nguvu huku machozi yakimlenga lenga usoni mwake.

“Ethan kwa hiyo una niacha mpenzi wangu?”

“Hapana baby siwezi kukuacha, ninakwenda kufanya tu majaribio ya kimpira nikifanikiwa basi nitakujiunga na kikosi cha vijana”

“Ethan kwa kipaji chako kweli una hisi kwamba huto fanikiwa mpenzi wangu?”

Swali la Camila likanifanya nikae kimya huku nikimtazama usoni mwake kwa maana, maandalizi yaliyo fanywa na timu ya Liverpool ni dhairi kwamba nime fanikiwa.

“Ukimya nao ni jibu Ethan, tazama nitabaki peke yangu, nitakaa na nani darasni?”

Camila alizungumza huku akimwagikwa kwa machozi, taratibu nikamkalisha kitandani huku nami pia nikikaa pembeni yake huku tukitazamana kwenye nyuso zetu.

“Camila usilie mpenzi wangu”

“Ethan nina umia. Haki ya Mungu nitamuomba babu anifanyie uhamisho nihamie huko Uingereza ili tuwe sote”

“Ila utamuomba mara baada ya mimi kufanikiwa?”

“Ndio”

Tukatazamana kwa sekunde kadhaa, nikajikuta nikipata msukumo moyoni mwangu wa kumbusu Camila lips zake. Taratibu nikamsogelea huku nikiwa nimeyafumba macho huku mapigo yangu ya moyo yakinienda kasi sana na jasho likinitiririka kwenye uso wangu. Tukaigusanisha midomo yetu, Camila akaongeza ujuzi zaidi kwa kuuingiza ulimi wake katikati ya lipsi zangu. Msisimko mkali ukaanza kunipanda, damu mwili mzima ikaanza kunienda kasi sana, nikaanza kuhisi uume wangu ukijaa na ukasimama kama vile ninavyo amka asubuhi. Camila akanilaza kitandani na kunilalia juu yangu huku tukiendelea kunyonyana midomo yetu. Camila akaanza kufungua vifungo vya shati lake jambo lililo nistua sana.

“Camila unataka kufanya nini!!?”

Niliuliza huku macho yakiwa yamenitoka sana.

“Ethan mimi ni nani yako?”

“Mpenzi wako”

“Nahitaji”

“Ehee”

“Ninahitaji penzi lako”

“Camila sisi bado n……..”

Camila akaizuia sentensi yangu kwa kiganja cha mkono wake wa kulia. Akashuka kitandani na kuusogelea mlango wa chumba changu na kuufunga kwa ndani. Akiwa hapo hapo mlangoni akavua nguo zake zote, jambo lililo yazidisha mapigo yangu ya moyo kuzidi kunienda kasi.

“CAMILA”

Nilizidi kubabaika kwa kulitaja jina la Camila, maneno yakaniishia na kujikuta nikiwa nimelegea mwili mzima, hata nikashindwa kumzuia Camila kunivua suruali yangu, akaimalizia boksa yangu na nikaushuhudia uume wangu ukiwa imesimama vizuri. Camila akaanza kuulama umme wangu na kuzidi kunilegeza mwili wangu. Raha ninayo ipata hakika sijawahi kuipata toka kuzaliwa kwangu hadi sasa nikiwa na umri wa miaka nane.

“Um…..ejifunzia wapi hivi”

Nilimuuliza Camila kwa shida sana huku macho yakiwa yamenilegea twepe tepwe.

“Nimeona kwenye laptop ya mama wakifanyana hivi na baba”

Nikazidi kujawa na kigugumizi, Camila taratibu akapanda juu ya mapaja yangu, akajipaka mate kidogo kwenye kitumbua chake, kisha taratibu akamkalia jogoo wangu na kujikuta nikitamani kutoa yote, kwani kitumbua cha Camila ni kigumu kidogo.

Nikamuona Camila naye sura ikiwa imejikunja sana mithili ya mtu anaye hisi maumivu. Nikamshuhudia jogoo wangu akizama kabisa kwenye kitumbua cha Camila.

“Haaa……”

Camila alitoa mguno huo na kunifanya nitazame kitumbua chake, nikashuhudia damu iliyo nifanya nikurupuke kwa haraka huku nikijaribu kumsogeza ila kutoka na kuishiwa nguvu nikajikuta nikishiwa kabisa na yeye akanirudisha chini.

“Damu Camila”

“Tamuu”

“Tamuuu wakati kunatoa damu!!”

Camila akaendelea kujinyanyua na kumkalia jogoo wangu kana kwamba hasikii ninacho muambia. Camila akaendelea kulifanya zoezi lake kwa dakika kama tano hivi, kisha akajilaza kitandani chali na kuniomba nipande juu yake. Akamshika jogoo wangu na kumuingiza ndani ya kitumbua chake kisha akanishika kiuno changu na kukiongoza katika kumsukuma jogoo wangu ndani na nje. Nikaanza kuzoea mchezo huu na kujikuta nikuongeza kasi na kumfanya Camila kutoa miguno niliyo hisi ni lazima nje itaweza kusikika.

“Nyonya hapa”

Camila aliniambia huku akionyesha kifua chake.

“Ninyonye nini?”

“Si ziwa langu?”

“Mbona hakuna chochote kifua kipo kama changu”

“Nyonya bwana”

Camila alizungumza kwa sauti ya kuhitaji kulia. Tukajikuta tukifanya mchezo huu kwa robo saa kisha, nikahisi jogoo wangu akiishiwa nguvu na kulegea kabisa.

“Asante Ethan”

Camila alizungumza huku akinikumbatia.

“Asante pia”

“Ethan ujue umesha weka ahadi la damu na mimi, nakuomba usifanye na mwanamke mwengine”

“Siwezi kufanya mpenzi wangu”

“Kweli?”

“Ndio”

“Ethan tambua kabisa mimi ndio mke wako wa badae, nina kupenda. Sijali tuna umri gani ila tambua kwamba nina kupenda na kukuhitaji”

“Asante mpenzi wangu. Ila mbona umetoka damu huku chini?”

“Umenitoa usichana wangu mpenzi wangu”

“Weee……!!”

“Ndio hata wew enimekutoa uvulana wako, au ulisha wahi kufanya na mwanamke yoyote hivi?”

“Hapana mke mpenzi wangu”

“Basi utambue ndio umesha niondolea usichana wangu”

Camila alizungumza huku akinitaza usoni mwangu. Tukastuka wote mara baada ya kuona shuka tulilo lalia kikiwa na doa kubwa la damu na mbaya zaidi shuka hili ni jekundu. Nikashuka kitandani huku nikifikiria juu ya kutoa shuka jengine kwenye droo na kulitandika. Camila naye akashuka kitandani, kitendo cha kusimama nikamshuhudia akianguka chini.

“Camila, Camila”

“Ehee….”

“Uana nini?”

“Nasikia maumivu kiunoni na miguu haina nguvu”

“Mungu wangu, jikaze”

Nilizungumza huku nikizidi kuchanganyikiwa, nikamnyanyua Camila huku nikiwa nimeshika kiuno chake. Camila akajaribu kupiga hatua mbili mbele ila akashindwa kabisa na kuniomba nimkalishe kwenye kiti cha pembeni, nikamkalisha huku jasho likizidi kunimwagika. Gafla mlango wa chumbani kwangu ukaanza kugongwa, ukarudiwa kugongwa mara ya pili.

“Camila ni mimi mama yako, muda wa kuondoka umefika sasa twende nyumbani”

Sauti ya mama Camila ikatustua sote wawili na kujikuta tukiutazama mlango huku Camila kushangaa sana kwani alikuja yeye mwenyewe, kwa haraka nikakimbilia dirishani, nikaona gari za zikiwa zimeongeka na kuwa tano huku baba Camila akiwa amesimama nje ya moja ya gari huku walinzi wakiwa wameimarisha ulinzi kila sehemu na lengo la kuja hapa ni kuondoka na mtoto wao.


Ujasiri wote ukanipotea, mwili mzima ukaanza kunitetemeka, nikamtazama Camila nikamuona akijitahidi kunyanyuka kutoka kwenye kiti alicho kikali.

“Camila itakuwaje mpenzi wangu”

Nilizungumza huku jasho likiendelea kuutawala mwili wangu.

“Ngoja”

“Mama nitarudi tu na walinzi?”

“Muda gani mwanangu?”

“Kama baada ya lisaa hivi”

“Ila baba yako ana hitaji kukuona”

“Muambie nitakuja tu mama”

“Sawa, kama umehitaji hivyo, ila hakikisheni munakuwa salama”

“Sawa mama”

Tukasikia vishindo vya mama Camila akiondoka katika eneo hili, kwa haraka nikafungua kisehemu kidogo katika mlango huu ambacho humsaidia mtu kuchungulia nje pale kunapo kuwa na mtu ana gonga mlango. Nikamshuhudia mama Camila akimaliza kukunja kona ya kuelekea katika ngazi za kushuka gorofani humu. Taratibu nikashusha pumzi huku nikiuegemea mlango huu.

“Wazazi wangu ni waelewa sana na wana nipenda sana”

“Hata kama Camila, hatujapaswa kufanya jambo kama hili”

“Ethan kumbuka kwamba wewe una ondoka na hisia zangu zinahisi kwamba huwezi kurudi, hivi kweli unahitaji mimi niendelee tu kuvumilia pasipo kukupa haki yako ya msingi”

“Camila ila kila kitu ni umri, kumbuka mimi na wewe hata miaka kumi na kitu hatujafikisha, ila mwenzangu ninaona una jua mambo mengi sana kuliko hata mimi”

“Ndio nina fahamu, kwani wewe hupendi mimi nifahamu?”

“Ninapenda, ila tungesubiri?”

“Hembu acha woga wako, njoo unisaidie kuninyanyua.”

Camila alizungumza huku akininyooshea mkono wake wa kulia. Taratibu nikaushika na kumnyanyua, mkono wangu wa kulia nikaupitisha kiunoni mwake, na taratibu tukaanza kutembea kuelekea kwenye mlango wa bafu lililomo humu ndani. Nikamkalisha kwenye sinki la kuogea kisha taratibu nikaanza kufungulia maji yenye uvuguvugu kwa maana kipindi hichi bariki katika nchi hii ya Ujerumani ni kali sana.

“Unajisikiaje?”

Nilimuuliza Camila huku nikiweka sabuni ya maji taratibu katika maji haya na kusababisha povu jingi.

“Nikajihisi nyonga zote zinaniwaka moto”

“Ila huu mchezo Camila ulio ufanya sio mzuri kwa umri wetu”

“Ethan nikuulize kitu?”

“Niulize?”

“Hujafurahia mimi kukupa wewe utamu?”

“Hee?”

“Hee nini hujafurahia?”

“Nimefurahi”

“Basi kaa kimya, mimi nitajua nini la kufanya. Na unaenda Uingereza, najua wewe ni mzuri na utakuwa maarufu sana, sasa ole wako nisikie una mwanamke mwengine haki ya Mungu nitamua huyo mwanamke. Sitaki kushirikiana na mwanamke mwengine kwenye penzi langu. Umenielewa Ethan?”

Camila alizungumza kwa msisitizo hadi nikapatwa na kigugumizi cha kumjibu.

“Ethan umenielewa?”

“Ndio nimekuelewa”

“Asante”

Tukaendelea kuoga huku akilini mwangu nikijitahidi kumfafanua Camila ili niweze kujua ni mtoto wa kike wa aina gani, ila ninashindwa kupata jibu kabisa. Tukatoka bafuni humu huku Camila nikiwa nimeshika mkono.

“Naomba shuka nikutandikie”

Camila alizungumza huku akitoa shuka hili, nikafungua kabati na kutoa shuka jipya na kumkabidhi, akalikunja kunja shuka hili tulio fanyia mapenzi na kuliweka juu ya kiti.

“Hivi unavyo tembea hivyo kwa kuchechema huogopi ukitoka nje?”

“Siwezi kuogopa kwani ni nani wa kuniuliza?”

“Camila mbona una jiamini sana? Wa kukuuliza si wazazi wako, au hao nao hawawezi kukuuliza?”

“Ethan ngoja nikuambie tofauti iliyopo kati ya wazazi wa kizungu na kiafrika. Sisi huku tunalindwa na mahakama, endapo itatokea mazizi akamchapa mtoto au akamfokea kwa ukali sana na mtoto akaenda kumstaki mzazi wake kwenye mahakama hiyo na mtoto akakiri kwamba mama au baba ame nyanyasa, basi mzazi anakabiliwa na kifungu cha jela na mtoto atakuwa chini ya uangalizi wa serikali. Ila kwa jinsi ninavyo fahamu wazazi wa Afrika kutokana na histori tunazo soma kwenye mitando, wao kumchapa mtoto wake na kumfokea ni jambo la kawaida sana na mtoto huwa hana sehemu ya kukimbilia kwenda kustaki”

“Ila ni kweli?”

“Ndio maana utakuta watoto wengi wa afrika, wanakuwa si rafiki kwa wazazi, kama ni baba ndio mkali basi watoto wana hamia kwa mama na kama mama ni mkali basi wote wana hamia kwa baba jambo ambalo sio zuri. Wote hupaswa kumuheshimu mtoto wao na kumlindia hisia zake”

“Haya nimekuelewa”

Camila akamaliza kutandika shuka hili kisha akanisogelea shemu nilipo simama huku nikiwa kama nilivyo zaliwa. Akaninyonya midomo yangu kwa sekunde kadhaa kisha mikono yake akaipitisha mabegani mwangu na kuikutanisha nyuma ya shingo yangu.

“Ethan hilo shuka nakuomba ulitunze, alama hiyo ya damu ni ukumbusho tosha wa kukumbua hii siku, ni siku moja kubwa sana kwenye maisha yetu ya mapenzi. Ikumbuke tafadhali mpenzi wangu”

“Sawa mpenzi wangu”

Camila akaanza kuvaa nguo zake, kisha nami nikavaa nguo zangu.

“Huo mwendo wako wa kuchechemea hakika una niogopesa”

“Usijali mpenzi wangu, nitajikaza tu”

“Hembu jitahidi kutembea tembea humu ndani basi, ili unipe matumaini”

“Jamani Ethan mbona hupendi kuniamini”

Camila alizungumza huku akianza kutembea katika chumba hichi, japo kidogo anaonyesha ana chechemea, ila akazidi kujikaza na kuzunguka zunguka katika chumba changu. Kutokana ni mimi ni mwana michezo nikamfanyisha mazoezi madogo madogo ambayo kwa jinsi nilivyo weza kuamini akafanikiwa kwa asilimia kadhaa.

“Ukijikaza kutembea hivyo hadi nje kwenye gari basi hakuna ambaye atakustukia kwamba wewe una tatizo”

“Sawa mpenzi wangu”

“Ninakupenda Camila na nimefanya hili tendo kutokana nina kupenda”

“Naamini unajua hisia na moyo wangu vipo wapi. Nakuomba ukajitunze”

“Sawa”

Tukanyonyana midomo yetu kwa dakika kadhaa, kisha tukatoka ndani humu huku nikimfwatilia kwa macho Camila hatu hadi tatua jinsi anavyo tembea. Tukafika sebleni na kumkuta bibi Jane Klopp akisoma moja ya kitabu amacho siku zote nimekuwa nikimuona akikisoma, ila sihitaji kumfwatilia.

“Ohoo Camila una kwenda sasa?”

“Ndio bibi”

“Karibu sana na usisite kuja kunitembelea hata kama mpenzi wako atakuwa hayupo”

“Sawa bibi”

Tukatoka nje, Camila akajikaza kutembea hadi kwenye gari lao. Mlinzi akamfungulia mlango na akaingia ndani na walinzi wengine wakaingia ndani ya gari la mbele kisha taratibu wakaanza kuondoka katika eneo hili.

‘Maisha bwana, katoto kadogo kana waamrisha mitu mikubwa’

Nilijikuta nikizungumza huku moyo wangu ukiwa umejawa na furaha, nikaingia sebleni bibi Jane Klopp akaniita wa ishara, nikamfwata hadi sehemu alipo kaa.

“Umemfanya nini mtoto wa watu?”

“Mama…….!!!”

“Ndio mimi kwa kukuangalia machoni natambua ni nini ulicho kifanya na huyu binti. Ethan kuwa makini mwanangu, nyinyi bado ni wadogo. Uhuru tulio wapatia tafadhali usiitumie vibaya ume nielewa?”

“Sawa mama nimekuelewa”

“Umemaliza kupanga nguo zako?”

“Ninitamalizia”

“Hakikisha una malizia. Ila muda mwengine Ethan narudia kuwa makini. Huyu ni mjukuu wa mtoto wa raisi, usijitafutie matatizo sawa”

“Sawa mama”

Kwa ishara bibi Jane Klopp akaniombe niondoke hapa sebleni, nikarudi chumbani kwangu na kitu cha kwanza nikalichukua shuka hili na kuliweka chini kabisa ya begi langu la nguo nitakalo ondoka nalo. Nikaweka kila kitu changu sawa. Mlango ukagonga, nikafungua na kumkuta Mery akiwa amesimama huku amebeba fuko kubwa.

“Nimekuletea nguo mpya hembu jaribisha”

“Asante dada”

“Usijali”

Nilaanza kujaribisha nguo hizi, kila nguo ambayo amenileta imenikaa mwilini mwangu vizuri na kunipendezesha. “Sasa ukienda huko Uingereza uonekane upo vizuri wewe ni maarufu sasa. Yaani hapa kila ninapo pita watu wananiuliza kweli Ethan ni mdogo wangu.”

“Unawajibuje?”

“Khaa ninawaambia ndio nimdogo wangu”

“Hahaaa”

Dada Mery akanisaidia kupanga nguo hizi mpya kwenye begi langu.

“Ethan, tambua kukua kwako kimichezo, usije ukasahau hii familia. Kumbuka kwamba sisi ndio ndugu zako, usije ukajisahau na kutokana na umaarufu ukajikuta ukatukana”

Dada Mery alizungumza kwa sauti ya upole sana huku akinitazmaa usoni mwangu.

“Nimekuelewa na siwezi kufanya hivyo dada?”

“Mungu akatungulie”

“Amen”

Tukatoka ndani humu, tukapata kwa pamoja chakula cha usiku kisha tukasali kwa pamoja wote watu wanne na tukarudi kwenye vyumba vyetu. Usiku kucha sikuweza kupata hata lepe la usingizi. Asubuhi na mapema nikaamka, nikaanza kujiandaa kwa safari. Nikatoka nje na kumkuta mzee Klopp naye akiwa tayari amesha jianda kwa kuvalia suti yake nya kijivu ambayo, kitendo cha kuiona moja kwa moja ikaikumbuka ndoti ya ajali ya ndege. Mzee Klopp meno yote thelathini yanaonekana mara baada ya kuniona. Nikamsalimia kwa heshima kubwa sana.

“Ngoja watoke hao wanawake watusindikize hadi uwanja wa ndege”

“Sawa baba”

Nilizungumza huku nikiweka begi langu juu ya moja ya meza. Baada ya dakika chache Bi Jane Klopp akatoka humu ndani.

“Mery bado hajatoka?”

Bibi Jane Klopp aliuliza huku akiwa amependeza kwa mavazi yake.

“Ndio mama”

“Nenda kamuite”

Nikapandisha ngazi, nikafika katika chumba cha dada Mery, nikagonga kwa muda huku nikimuita dada Mery jina lake. Dada Mery akaniruhusu kuingia ndani ya chumba hichi. Nikastuka sana mara baada ya kumkuta dada Mery akiwa yupo uchi kama alivyo zaliwa huku akijipaka mafua mwili wake.

“Mbona umes tuka?”

“Mmmmm?”

“Njoo ninipake mafuta huku mgongoni”

“Ila dada unge vaa kidogo”

“Nivae kidogo wapi. Njoo au kwa udogo huo unaweza ukanibaka mimi dada yako?”

Nikatingisha kichwa nikiashiri kwamba siwezi kumfanyia kitendo kama hicho.

“Basi njoo unipake.”

Huku mwili ukinitetemeka nikaanza kutembea kumfwata dada Mery hadi katika sehemu ya kioo kikubwa. Akaniweka mafuta kiasi kidogo kwenye kiganja changu cha mkono wa kulia, kutokana ni mrefu kiasi, akainama kidogo na kunifanya nizidi kuona kitumbua chake.

Nikaanza kumpaka mafuta hayo taratibu kwenye mgongo wake huku nikianza kuhisi fujo za jogoo wangu jinsi anavyo furukuta ndani ya boksa yangu.

“Jana ulimfanya nini Camila?”

“Ehee?”

“Ethan mdogo wangu niambie ukweli jana ulimfanya nini Camila?”

“Sijamfanya chochote?”

“Ethan ni mara ngapi huwa nina kuambia kwamba sipendi uongo?”

“Ni mara nyingi”

“Sasa kwa nini una nidanganya. Hembu niambie ukweli”

Dada Mery alizungumza huku akiushika mkono wangu wa kulia, akakigusisha kiganja changu kwenye kitumbua chake na kuana kikichezesha chezesha. Japo ni baridi kali, ila jasho halikusita kunitoka mwilini mwangu. Dada Mery akafika mbali zaidi mara tu ya kukiingiza kidogo changu cha katikati katika kitumbua chake na taratibu akaanza kukikatikia kiuno huku mkono wake mwengine wa kushoto akiupitisha pitisha kichwani mwangu na kunifanya nijawe na hisia kali sana.

“Nyinyi NGURUWEEE munafanya nini ndani ya nyumba yangu?”

Tuliisikia sauti ya ukali ya mzee Clopp iliyo nifanya nikurupuke kutoka katika tukio nililo kuwa nina lifanya hadi kuanguka chini huku macho yangu yakimtazama mzee Clopp jinsi alivyo vimba kwa hasia kali kama chui aliye uliwa mwanaye.



Mzee Klopp akaanza kunifwata kwa hasira, ila dada Mery akamuwahi na kumzuia baba yake.

“Ethan nenda nje”

Dada Mery alizungumza na kunifanya ninyanyuke kwa haraka na kukimbilia sebleni. Bibi Jane Klopp akabaki akinishangaa jinsi ninavyo hema.

“Kuna nini?”

Bibi Jane aliniuliza huku akinitazama machozi mwangu, kwa jinsi nilivyo jawa na woga nikajikuta hata nikshindwa kabisa kumjibu bibi Jane Klopp. Kelele za kufoka za mzee Klopp zikamfanya bibi Jane Klopp kuanza kupandisha ngazi kuelekea gorofani. Kwa haraka nikatoka katika mlango wa kutokea humu ndani na nikaanza kukimbia kuelekea getini.

“Ethan vipi mbona una kimbia kuna nini?”

Mlinzi aliniuliza huku akinitazama.

“Kuna mtu ninakwenda kuonana naye hapo mbele tafadhali ninakuomba unifungulie geti”

Mlinzi akaminya batani ya kufungua geti hili, iliyopo ndani ya kibanda chake. Nikaanza kukimbia kuelekea mtaani, kutokana mji huu nimeufahamu kwa asilimia kubwa, hakuna hofo ya mimi kuweza kupota. Nikazidi kutokomea mtaani huku nikiamini kwa kufanya hivi kutasaidia yale mabaya ambayo Ethan alinieleza juu kuuwawa kwa mzee Klopp basi hayato tokea tena.

“Ethan naomba unisaidie”

Nilizungumza huku nikizidi kusonga mbele, nikikatiza katiza kwenye mitaa japo kuna baadhi ya watu ambao walinikodolea macho, nina hisi wengi wao watakuwa wakinifananisha kwa maana katika umri wangu huu mdogo nimeweza kuwa maarufu sana.

‘Hei’

Nilimuona Ethan pembeni yangu akitembea pamoja nami.

‘Nimeondoka nyumbani kwa ajili ya lile tatizo lisitokee’

‘Natambu hilo, pia ni maamumuzi mazuri’

‘Sasa natakiwa kwenda wapi?’

‘Wewe unataka kwenda wapi?’

‘Sijui na siwezi kurudi kwa yule mzee kwa maana ni aibu kubwa sana mimi kukuta nikifanya vile na yule dada’

‘Hata dada yako hakutarajia kufanya vile ila nilimtuma jini mahaba, kumuingia na kujikuta akikutamani na kufanya vile.

‘Haukuona njia nyingine ya kuweza kufanya hadi unifanyie vile?’

‘Ni njia gani nyinyine ya kufanya sasa?’

‘Ethan hembu niambie basi maisha yangu ya mbeleni yatakuwaje?’

‘Siwezi kukuambia na mimi sio mtabiri wako. Ninakueleza pale unapo kuwa na tatizo kubwa ambalo litakuhatarishia maisha yako, ila kwa sasa siwezi kukuambia chochote’

Maneno ya Ethan yakanikatisha tamaa kwa kweli. Nikasimama na kutazama majengo mengi yaliyo tuzunguka katika eneo hili.

‘Ili kufanikiwa ni lazima uweze kuitambua shida, shida itakayo kujenga kiakili, kimaarifa na utaweza kuwa makini na mafanikio yako kwa maisha yako ya baadae’

‘Mmmmm’

‘Ndio’

Ethan akapotea kwenye uwepo wa macho yangu. Nikatazama nilipo nikashusha pumzi nyingi kisha nikaendelea na mizunguko katika jiji hili la Berlin. Hadi inaitimia usiku wa saa moja sikuweza kupata chochote tumboni mwangu na wala sifahamu ni wapi nitalala katika usiku huu. Nafsi moja ina nishauri niweze kurudi kwa mzee Klopp, ila nafsi nyingine ina nishauri nisiweze kurudi kabisa nyumbani kwa mzee Kloop kwani kwa hasira aliyo nayo juu yangu ni lazima atania. Baridi kali ikazidi kunitesa na kuusumbua moyo wangu, hakika katika hali ngumu ya maisha niliyo ipitia moja wapo ni hii. Nikatamani kuyafuta japo kibanda cha simu niweze kumpigia mpenzi wangu Camila aweze kunisaidia, ila nikaona sio jambo la burasa kwa mimi kuwa omba omba na pia atahitaji kufahamu ni sababu gani ambayo ilinifanya mimi kuweza kuondoka katika nyumba ya mzee Klopp na endapo ataifahamu ni sababu ya kimapenzi nahisi hata msaada wake kwangu naamini unaweza kubadilika. Nikiwa katika moja ya godauni kubwa ambalo lina watu wengi omba omba wanao lala, nikaona kundi kubwa la vijana walio nizidi umri wakinisogelea. Woga ukanijaa na nikaanza kurudi rudi nyuma, ila kwa wingi wao wakafanikiwa kunizunguka na kuniweka katikati.

“Hei umefwata nini hapa wewe mtu mweusi?”

Mmoja wao alizungumza huku akinisukuma.Nikashindwa kuwajibu chochote zaidi ya kuendelea kutetemeka kwani katika maisha yangu kitu nisicho kipenda ni kupigana na wala sina ujuzi wowote katika swala la kupigana.

“Hujibu si ndio?”

“Mi…..”

Nikastukia ngumi nzito ikitua kwenye shavu langu la upande wa kulia na kunifanya niweweseka na kuona maruwe ruwe mengi sana ambayo hakika yakanipotezea hata uwezo wa kuweza kuona vizuri. Nikastukia mtama mzito ulio niangusha chini mzima mzima. Wakaanza kunivua viatu, wakafwatia surualia yangu pamoja na tisheti niliyo ivaa na wakaanza kunipiga mateka mfululizo. Nikaendelea kujikunyata ili wasiniumize uso wangu, galfa nikahisi kitu chenye ncha kali kikinichoma kwenye mbavu zangu, jamgo lililo nifanya nipige kelele kali sana za maumivu kwani maumivu yake ni makali kupita hata mateke na ngumi wanazo nipiga.

“Hei muna mfanya nini mwenzenu”

Vijana hao mara baada ya kusikia kelele hiyo, wakatawanyika na kukimbia na kuniacha nikiwa nimelala chini huku nikilia kwa uchungu sana. Nikajaribu kuuepeleka mkono wangu wa kulia kwenye mbavu zangu, nikajikuta nikiwa na kisu kikiwa kimezama kwenye mbuvu zangu jambo liilo nifanya nichanganyikiwe sana na kuzidi kulia, hadi nikapoteza fahamu.

***

“Hei ume amka?”

Nilisikia sauti ya kime ikipenya vizuri masikioni mwangu. Nikamtazama mwanaume anaye nisemesha, nikamuona ni mwanaume mwenyea asili ya kiafrika kama mimi. Mwanaume huyu kichwani mwake ana rasta nyingi na defu. Mkononi mwake ameshika msokoto mkubwa wa bangi na katika chumba hichi nilicho lala kimejaa mapicha picha mengi ya mwanamziki Bob Marley.

“Nipo wapi?”

Niliuliza kwa upole sana huku nikimtazama jaa huyu, kabla ya kunijibu akapiga fumba moja la bangi aliyo ishika kisha akapuliza hewani na kukohoa kidogo huku akipiga piga kifua chake.

“Dogo upo kwa rasta Man Bob….Wooo, Wooo”

Mwanaume huyu alizungumza huku akirusha rusha nywele zake, nikajitazama nilipo lala. Ni kitanda kimoja kidogo na kina mashuka yanayo nuka kwa uvundo wa kuto kufuliwa kwa siki ningi. Eneo la tumboni mwangu nimezungushiwa bandeji moja kubwa sana.

“Unajisikiaje?”

Aliniuliza huku akivuta kistuli na kukaa pembeni yangu. Taratibu nikanyanyuka na kukaa kitako huku nikimtazama.

“Ninajisikia maumivu”

“Ohoo vuta kitu hichi kidogo, utajisikia poa kabisa”

“Hapana asante”

Mwilini kitu nilicho baki nacho ni boksa tu.

“Nipo hapa toka lini?”

“Jana usiku, nilikuokoata kuna madogo walikuwa wanakushambulia”

“Nahitaji kurudi nyumbani”

“Nyumbani?”

“Ndio”

“Kwenu ni wapi?”

Nikajikuta nikishindwa kumjibu rast man huyu mara baada ya kuona taarifa ya kutafutwa kwangu kwenye tv ndogo ya chogo iliyomo ndani humu na endapo mtu atatoa ushirikiano wa kupatikana kwangu atapatiwa dola elfu hamsini na familia yangu. Rasta Man huyu akanitazama vizuri, kisha akarudisha macho yake kwenye tv ili kunifananyisha na kile alicho kiona.

“Ahaa wewe ndio Ethan Klopp?”

Nilimjibu rasta man huyu kwa kutingisha kichwa kwamba ndio mimi. Akaruka juu kwa furaha, kwa haraka akata simu yake mfukoni na kuanza kupiga namba za mzee Klopp zinazo onekana kwenye tv.

“Woo wooo rasta mana Bob hapa nina ongea na mzee Klopp mgongoni namba saba machachari”

Rasta man huyu alizungumza kwa shauku kubwa, naamini akili yake hapo ina furahia donge nono lililo ahidiwa na familia ya mzee Klopp.

“Kijana wenu nipo naye, na hali yake sio nzuri. Ila hakikisheni kwamba muna kuja na mpunga wangu kumchukua la sivyo hamta muona”

“Sijamteka mimi, ila nilimsaidia, mikiwa tayari nipigieni simu muje kumchukua”

“Poa poa, wooo wooo rasta mana weeeee”

Alikata simu huku akiwa amejawa na furaha kubwa sana. Mawazo mabaya juu ya adhabu ambayo ninaweza kupewa na mzee Klopp, yakaanza kunitawala kichwani mwangu. Rasta man huyu akazidisha makeke ya kunisaidia, ili maradi niweze kumuona mwema. Baada ya dakika kama kumi hivi simu yake ikaita kwa haraka akaipokea na kuiweka sikioni mwake.

“Ndio, nipo naye hapa. Chukua uzungumze na mama yako”

Rasta man akanikabidhi simu yake taratibu nikaipoke na kuiweka sikioni mwangu.

“Ethan”

Niliisikia sauti ya bibi Jane Klopp akiniita huku analia.

“Naam mama”

“Ohoo asante Mungu, unaendeleaje mwanangu?”

“Naumwa mama”

“Ohoo Mungu wangu tunakuja sasa hivi sawa”

“Sawa mama”

Simu ikakatwa, nikamrudishia rasta man. Kwa haraka masta man akaanza kufanya usafi ndani kwake humu, huku mifuko ambayo imejaa misokoto ya bangi akiitoa nje na wala sifahamu ni wapi alipo iweka. Baada ya muda rasta man akaingia ndani humu huku akiwa ameongozana na bibi Jane Klopp pamoja na askari wawili. Bibi Jane Klopp kwa haraka akanikimbilia na kunikumbatia, alipo liona jeraha lililopo kwenye mbavu zangu kwa haraka akapiga simu hospitali na haukupita muda mrefu gari la wagonjwa likafika. Madaktari wakaniweka juu ya machelea maalumu huku waandishi wa habari nao wakijitahidi kuchukua tukio hili. Rasta man akaninyooshea dole gumba, ikiwa ni ishara ya kunitakia safari nje.

Njia nzima bibi Jane Klopp anasali huku machozi yakimwagika usoni mwake. Madaktari wakaanza kunihudumia jeraha langu upya kabisa. Tukafika hospitalini na nikashushwa kwenye machela hii kwa haraka nikakimbizwa kwenye chumba cha upasuaji huku bibi Jane Klopp akizuiwa kuingia ndani ya chumba hichi. Nikachomwa sindano ambayo ndani ya muda mchache nikajikuta nikiishiwa nguvu mwilini mwangu na kulala usingizi fofofo.

***

Cha kumshukuru Mungu upasuaji umefanyia vizuri na kisu nilicho chomwa hakikuni athiri sana katika pamvu zangu. Watu mbalimbali ndani ya nchi hii ya Ujerumani, hawakusita kufika hospitalini hapa kunijulia hali kwani tayari nimezidi kuwa maarufu. Camila na wazazi wake nao hawakuwa nyuma kunitembelea kila siku huku wakionyesha dhairi kwamba wamenikubali kama mkwe wao japo mimi na mtoto wao bado tuna umri mdogo ambao hatupaswi kuingia kwenye mahusiano.

“Ethan”

Mzee Klopp aliniita huku akiwa amekaa pembeni ya kitanda changu.

“Naam baba”

“Ninakuomba unisame kwa kila kitu ambacho kimetokea kwenye maisha yangu. Natambu hasira yangu na kung’ang’ania kwangu uwe mchezaji kutokana na tamaa ya kipesa ndio kumekufanya leo hii uwe hapa kitandani. Naomba unisamehe sana”

Mzee Klopp alizungumza kwa unyonge na kwa upole sana na kumfanya Bi Jane kunitazama usoni mwangu.

“Nimekusamehe baba naombeni na mimi munisamehe, nimewapa hasara ya kifedha”

“Hapana hapana Ethan, pesa sio kitu, ila uhai wako ndio kitu muhimu kwenye maisha ya hivi sasa”

Bibi Jane Klopp alizungumza huku akinishika mkono wangu wa kulia.

“Kwa sasa tutakuacha uendelea na mashomo yako na endapo hadi utakapo maliza elimu ya msingi basi unaendelea na hili swala la kufikiria kucheza katika timu kubwa”

“Nashukuru sana baba kwa kuelewa”

Muda wa mzee Klopp na mkewe kukaa ndani humu chumbani kwangu ukaisha na wakaondoka na wakaniacha mimi peke yangu kama siku zote na uangalizi wote hufanywa na madaktari.

‘Za masiku’

Niliisikia sauti ya Ethan, nikatazama kwenye kona moja ya chumba hichi nikamuona akiwa ameiegemea huku akinitazama.

“Siku zote ulikuwa wapi?”

“Kwani nilikueleza kitu gani?”

“Sawa, kunieleza kutu hichi ndio kukufanya uondoke na kuniacha peke yangu kwenye matatizo na ona sasa jinsi nilivyo jeruhiwa”

Nilizungumza kwa jazba kidogo huku nikimtazama Ethan.

“Wooo sasa kwa nini usipambane na wale vijana?”

“Ethan hembu acha kunitania bwana. Uliniambia kwamba utanipa nguvu sasa nguvu zenyewe mbona sizioni?”

“Kwani umesha kuwa?”

“Hata kama, ila nahitaji wale vijana nao niwafanye kitu kibaya”

“Kweli?”

“Ndio”

“Twende”

“Wapi?”

“Si sehemu walipo ukawafanyie kitu kibaya”

“Si unaona kabisa nina jeraha”

“Huniamini au?”

Nikamtazama Ethan kwa muda kidogo, kisha nikachomoa sindano inayo ingiza maji kwenye mishipa yangu. Nikashuka kitandani, Ethan akanikumbatia kwa kasi ya ajabu tukatoka katika eneo hili la hapo hospitalini na kuanza safari ya kwenda eneo walipo vijana amabo walinipiga na kunichoma kisu changu katika mbavu zangu.


Kwa uwezo wa Ethan, ndani ya muda mchache tukafika katika moja ya jumba bovubovu ambalo kidogo lipo nje ya mji.

“Hapa ndipo wanapo ishi?”

“Ndio”

Ethan alizungumza huku tukisimama nje ya mlango wa kuingilia. Taratibu Ethan akaanza kugonga mlango huu.

“Sasa kwa nini tunagonga”

“Unahisi tukiingia kwa staili tulio ijia unahisi watakutambuaje, kesho si watasema wewe ni jini, ikiwa jini ni mimi”

“Mmmh”

“Yaa, tena ninaingia ndani ya mwili wako”

Ethan akapotea kwenye uwepo wa macho yangu. Mwili mzima ukanisisimka na kujihisi ni mtu mwenye nguvu sana. Mlango ukafunguliwa, akasimama kijana ambaye kwa haraka niliweza kumtambua kwani yeye ndio aliye anza kunisemesha siku walipo nivamia.

“Hei wewe mtu mweusi umekuja kufanya nini hapa?”

Jamaa alizungumza kwa dharua. Nikamsukumia ndani, nikashangaa kumuona jamaa akipaishwa kimo cha mbuzi na akatua kwenye moja ya meza na kuiangukia hadi ikavunjika vunjika jambo ambalo liliwastua wezake wengine.

“Ni useng** gani huuu”

Mwenzao mmoja alizungumza huku wakiacha kucheza game ya mpira kwenye tv iliyopo hapo sebleni na kunifwata. Woga na wasiwasi kama nilio kuwa nao kwa siku ya kwanza wote umeniondoka, maumivu kwenye jeraha langu sikuweza kuyahisi kabisa mwilini mwangu. Kuna kijana humu ndani akaokota kitu chake kuhakikisha kwamba ana nivamia.

Wakaanza kunishambulia ila kila walivyo jaribu niliweza kuwadhibiti kisawa sawa na kila niliye mpiga ngumi aliambulia ngumi au teke lililo wapelekea kuvunjika katika sehemu hiyo ambayo nitampiga. Ndani ya muda mfupi vijana wote nane nikafanikiwa kuwadhibiti na kila mmoja ana ugulia maumivu huku wengine wamepoteza fahamu.

“Unatakiwa kuwaua ili siri yako isitoke”

Niliisikia vizuri sauti ya Ethan masikioni mwangu.

“Ethan kuua ni dhambi”

“Watakuua wewe siku, waue wote”

Ethan alizungumza kwa ukali, nikawatazama vijana hawa jinsi wanavyo pata shida ya maumivu. Roho ya kuwaua ikaanza kunijaa. Huruma ya kibinadamu ikafutika kabisa, nikaanza kuwavunja shingo mmoja baada ya mwengine. Zoezi la kuwaua halikumaliza dakika hata tano.

“Kazi nzuri”

Ethan alizungumza huku akitoka mwilini mwangu.

“Ngoja nifute ushahidi wote”

Ethan alizungumza huku akizikusanya maiti hizi na kuziweka eneo moja. Akanyoosha mkono wake wa kushoto, nikastuka sana mara baada ya kuona ukitoa moto mwingi ulio sababisha maiti za vijana hawa kuanza kuwaka. Tukatoka nje na Ethan kwa uwezo wake wa kijini akaendelea kuichoma nyumba hii na kuwaka moto mkubwa sana. Kama tulivyo kuja hapa ndivyo tulivyo rudi hospitalini na hakuna nesi aliye weza kugundua.

‘Ninaondoka ila hakikisha kwamba siri ya mauaji humuambii mtu wa aina yoyote hata Camila mwenyewe sawa’

“Sawa”

Ethan akaondoka katika eneo hili. Kupitia tv iliyomo humu ndani kwangu, nikaona taarifa juu ya kuungua kwa jumba moja lililopo nje ya mji huku ikisadikika kuna watu wemeungulia ndani ya nyumba hiyo. Taarifa hii kidogo ikanipa wasiwasi kwa maana watendaji wa tukio hilo ni mimi na Ethan.

Asubuhi taratibu zikaendelea kama kawaida, madaktari wakanitembelea na kunichoma sindano za kukausha kidonda. Baada ya wiki moja nikaruhusiwa kutoka hospitalini hapa nikiwa na afya yangu nzuri kabisa. Nikakaa siku chache nyumbani kisha nikarudi shule kuendelea na masomo yangu ya darasa la pili. Kurudi kwangu shule imekuwa ni furaha kwa waalimu na wanafunzi wezangu. Maasomo yakazidi kusonga mbele huku ushiriki wangu kwenye michezo ukizidi kuinyanyua shule kwenye mashindano mbali mbali ndani na nje ya nchi ya Ujerumani. Ufauliji wangu katika masomo nao ukazidi kunifanya niwe kipenzi cha wanafunzi wengi sana, huku Camila kadri ya siku zinavyozidi kwenda ndivyo jinsi tulivyo jikuta tukizama kwenye penzi letu.

***

Nikiwa na umri wa miaka kumi na mbili nikamaliza elimu ya msingi na nikachaguliwa kwenda shule ya vipaji maalumu huku Camila akichaguliwa kwenda katika shule nyingine ya jinsia moja ya kike ila ni karibu sana na shule yetu hii ya kiume. Nikiwa kidato cha pili, nikaletewa maombi mengine ya kujiunga na timu nne kubwa za mpira ambazo ni Liverpool, Real Madrid, Bacelona na Beyurn Munich.

“Ethan unaitwa”

Mwenzangu mmoja aliniita nikiwa bwenini nikipitia pitia baadhi ya mikataba niliyo tumiwa kwa njia ya barua pepe na mameneja wa timu hizo kwani kipaji changu cha mpira kimekuwa kikubwa kwa hali ya juu.

“Na nani?”

“Mkuu wa shule”

Nikarudisha mikataba hii ndani ya kabati langu, nikalifunga kisha nikaanza kuongozana na kijana huyu kuelekea kwa mkuu wa shule. Nikaingia ofisini kwake na kumkuta akiwa peke yake. Nikamsalimia na akaniomba niweze kukaa kwenye kiti kilichopo pembeni ya meza yake.

“Samahani kwa kukutoa kwenye mapumziko yako”

“Hakuna tabu mwalimu”

“Kuna taarifa imekuja hapa sio njema kidogo kwako na wala kwetu”

Nikajiweka vizuri kwenye kiti huku nikimtazama mwalimu mkuu usoni mwake.

“Nimepokea simu kutoka nyumbani kwenu na dada yako ndio alinipigia”

Mapigo ya moyo yakaanza kunienda kasi huku nikimtazama mkuu wa shule.

“Unatakiwa kwenda nyumbani sasa hivi kwa maana hali ya mzee wako haipo vizuri sana. Tumekuandalia helicopter ya shule na itakuepeleka hadi nyumbani kwenu”

Nikashikwa na kigugumizi na nikashindwa hata kujua ni kitu gani ninaweza kukizungumza, kwani mzee Klopp ni zaidi ya baba kwangu, kwa maana amekuwa ni mpiganaji na ni mtu ambaye amenifunza mambo mengi sana hususani kwenye maisha ya mpira. Nikiwa katika hali ya bumbuwazi, akaingia sekretari wa shule.

“Mkuu helicopter ipo tayari kwa kuondoka”

“Sawa, nenda na Ethan hakikisha kwamba humuachi peke yake hadi pale atakapo fika nyumbani kwao”

“Sawa mkuu”

Tukatoka ofisini humu na moja kwa moja tukaelekea katika kiwanja cha helicopter. Tukaingia ndani ya helicopter hii na taratibu tukaanza safari ya kuelekea nyumbani huku akili yangu ikijaribu kutengeneza picha ya hali ya nyumbani nitakavyo ikuta. Akili yangu moja inaniambia kwamba mzee Klopp amefariki huku akili yangu nyingine inaniambia kwamba mzee Klopp yupo hai.

‘Ethan upo wapi rafiki yangu’

Nilimuita Ethan kimoyo moyo pasipo hata sekretari wa shule kuweza kusikia kitu chochote. Ndani ya dakika kumi na tano tukafika katika jumba la mzee Klopp ambapo napo kuna uwanja wa helicopter, nikafunguliwa mlango na mmoja wa walinzi wa jumba hili la mzee Klopp, nikashuka na nikaanza kukimbia kuelekea ndani ya jumba hili.

Ukimya nilio ukuta sebleni ukanistua sana, kwa haraka nikapandisha ngazi kuelekea gorofani, nikakutana na madaktra wawili kwenye kordo wakizungumza na dada Mery.

“Ethan”

Dada Mery aliniita huku kwa haraka akinifwata na kunikumbatia kwa nguvu huku akilia kwa sauti ya chini sana

“Baba yupo wapi?”

“Yupo chumbani”

Sikutaka hata kuulizia hali yake ipo vipi kwa haraka nikaingia ndani ya chumba cha mzee Klopp, nikamkuta akiwa amewekewa mashine za kupumulia huku pembeni yake akiwa amekaa bibi Jane Klopp. Bibi Jane Klopp taratibu akanyanyuka huku akinitazama usoni mwangu. Macho yake yamebadilika rangi na kuwa mekundu sana, anaonekana ni mtu ambaye alikuwa akilia kwa muda mrefu sana. Bibi Jane Klopp akanikumbatia kwa muda huku akilia. Mzee Klopp akanitazama kwa muda huku akihema kwa shida sana, kwa ishara ya mkono wake wa kulia akaniita. Nikamuachia bibi Jane Klopp na kumfwata mzee Klopp kitandani alipo lala.

“Eth…a….”

Mzee Klopp aliniita kwa shida sana, machozi yakaanza kunimwagika usoni mwangu.

“Ndio baba”

“M…ua…an..ngalie mama yak….o na dada yako”

“Mimi…..ni….nakufaa, ila hakikisha kwamba unatimiza ndoto zako sawa mwanangu?”

“Sawa baba”

“Makampuni yote yapo chini yako, wewe ndio mmiliki na nilisha weka kila kitu kwa mwana sheria hakikisha kwamba unayaongoza katika msingi na msimamo mzuri. Hakikisha kwamba huyumbishwi na umri wa mtu yoyote sawa”

Mzee Klopp alizunugmza kwa kujikaza sana

“Sawa baba”

Mzee Klopp akanitazama kwa muda kidogo, kisha akaniomba niweze kumkumbatia. Taratibu nikamuinamia na kumkumbatia. Kwa ishara mzee Klopp akamuita mke wake naye akamuomba amkumbatie, nikatoka nje na kumuita dada Mery akaingia chumbani humu tukawakuta bibi Jane Klopp na mume wake wakiwa wamekumbatiana huku wote wakiwa wanalia kwa uchungu sana. Dada Mery naye akajumuika mama yake katika kumkumbatia baba yake.

Mlio wa mashine ya kumsaidia kupumua, ikaanza kutoa mlio mithili ya alarm. Jambo lililo tufanya tushtuke sana na kuogopa kwa haraka wakaingia madaktari na wakamuomba bibi Jane Klopp na mwanaye wamuachie mzee huyo. Madaktari kwa kutumia mashine maalumu wakaanza kumstua kifuani mzee Klopp. Mashine hizo hazikuweza kufanya kazi kwani bado kijimstari cha rangi nyekundu kinaonekana kwenye mashine hiyo.

Madaktari wakajitahidi kulifanya zoezi hilo ndani ya dakika tano, kisha wakatugeukia huku wakiwa na sura za masikitiko sana. Daktari mmoja akatingisha kichwa akiashiria kwamba mzee Klopp hatupo naye tena duniani. Nikamshuhudia bibi Jane Klopp akianguka chini na kupoteza fahamu. Dada Mery akajitahidi kwa uwezo wake kuhakikisha kwamba hapati mstuko, ila bumbuwazi lililo mpata hakika limemfanya abaki amekaa pembeni ya mwili wa marehemu pasipo kufanya jambo lolote.

Kwa kusaidiana na madaktari hawa wawili tukasaidiana kumnyanyua bibi Jane Klopp na kumlaza kwenye moja ya sofa na akaanza kumpatia huduma ya kwanza. Hali ambayo inayo endelea ndani humu hakika imenifanya nami niwe nimekaa njia panda, hakika sijui nianzie wapi, kwani kila linalo endelea ninahisi ni kama muujiza ambao natamani siku zirudi nyuma ila ninashindwa.

“Ethan”

Daktari mmoja aliniita kwa ishara tukatoka nje ya chumba hichi.

“Mzee ameondoka duniani, wewe kama mwanaume hivi sasa tunakutegemea kuweza kutoa kauli ya familia kama mwanaume. Dada yako ndio kama vile unavyo muona alivyo. Mama naye ndio kama vile, tunakusikiliza”

Maneno ya daktari huyu yakanifanya nimkodolee tu macho na kushindwa hata kumjibu jambo la aina yoyote.

“Ethan”

“Naam”

“Umenielewa kitu ninacho hitaji kukizungumza”

“Ndio nimekuelewa”

“Jiandae katika hilo na tunahitaji mwili wa mzee kupelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti kabla haujaanza kuharibika”

“Ngoja kwanza kwani mzee alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa gani?”

“Saratani ya damu ndio ilikuwa inamsumbua”

“Kwa nini sikuweza kuambiwa hadi leo amefariki ndio ninaambiwa hili jambo?”

“Mzee mwenyewe alihitaji usiambiwe”

“Kwa nini?”

“Kwanza ni kutokana na umri wako, pili ni kutokana na masomo.”

Nikafumba macho yangu taratibu kisha nikayafumbua.

“Hakikisheni kwamba habari ya kufa kwa baba haivuji hadi pale nitakapo wambia sawa”

“Sawa Ethan”

Nikarudi ndani ya chumba hichi na kumshika mkono dada Mery na kutoka naye ndani humu. Tukaingia chumbani kwangu, Mery akanikumbatia kwa nguvu na kuanza kulia kwa uchungu sana, nikaanza jukumu la kubembeleza taratibu.

“Ethan kweli baba amekufa”

“Yaa amekufa, ila nakuomba ujikaze sasa”

“Eheee”

“Nahitaji ujikaze nitazame nitazame”

Nilizungumza huku nikimshika dada Mery mashavuni mwake. Tukatazamana kwa sekunde kadhaa.

“Sisi ndio tulio baki sasa, tujikaze na tushirikiane katika hili, ukiniacha mimi mwenyewe katika hili nitashindwa sawa dada yangu”

“Ehee”

“Sasa sikia kitu kimoja, nahitaji niweze kupata kitabu cha orodha ya mameneja wote wa kampuni za mzee na wale wanasheria wake wawili. Si unafahamu kitabu kilipo?”

“Ndio”

“Twende ukanipatie”

Tukatoka katika chumba changu na kuelekea katika ofisi ya mzee Klopp. Dada Mery akafungua moja ya kabati, tukaona shelf ya chumba akaingiza namba za siri ambazo niliweza kuziona. Akafungua mlango na akatoa kitabu hicho chenye majina na namba za simu za watu wote ambao ni wasimamizi wa makampuni ya mzee Klopp ambayo ni zaidi ya kumi na mbili. Nikaanza kazi ya kumpigia kila mmoja na kumuomba aweze kufika katika nyumba ya mzee Klopp haraka iwezekanavyo kwani kuna kikao cha dharura. Ndani ya lisaa moja mameneja kumi na mbili pamoja na wanasheria wawili wakafika nyumbani humu, huku kila mmoja akishangazwa na wito wangu, kwani haukuwa ni wito wa kubembeleza zaidi ya kuwa wito wa kuamrisha.

“Kijana mdogo inakuwaje unatuita kwa kutuamrisha?”

Mzee mmojaa alizungumza kwa kufoka huku wakiwa wamekaa sebleni hapa.

“Mzee kabla sijamaliza kuzungumza nilicho waitia kuanzia hivi sasa huna kazi”

Maneno yangu yakawafanya watu wote kustuka sana, hata dada Mery mwenyewe akaonekana kustushwa kwani maamuzi yangu hakuna hata mmoja aliye yataarajia kwamba nitayatoa hivyo.



“Sina kazi, wewe ni nani ambaye unanisimamisha kazi”

Mzee huyo alizungumza kwa ukali sana huku akinitazama usoni mwangu. Mwanasheria wa familia akasimama.

“Samahani kwa kuweza kuwaingilia katika hili, ila nina jambo ninaomba niweze kulizungumza na kuliweka sawa kwenu nyote.”

Mwanasheria akafungua brufcase yake na kutoa faili moja jeusi.

“Hili hii faili jeusi, nina amini nyinyi nyote humu ndani munaweza kutambua na kuelewa ni kitu kinacho husiana na faili hili. Huyu ni Ethan Klopp, ni mtoto wa mwisho wa mzee Ethan. Mikaka miwii iliyo pita kabla ya tarehe ya leo mzee Klopp aliweza kuniita ofisini kwake na kunipa hii fomu hapa ambayo ni nguvu ya urithi”

“Mzee Klopp kwa akili zake yeye mwenyewe na ufahamu wake yeye mwenyewe pasipo kulazimishwa na mtu wa aina yoyote, aliweza kuacha urithi huu kwa kijana huyu Ethan Klopp. Urithi huu unampa Ethana nguvu ya kumiliki kila mali ambayo mzee Klopp ana miliki. Makapuni na majumba yote yapo chini ya Ethan. Hivyo naomba muweze kumsikiliza kijana huyu”

Mwanasheria mara baada ya kumaliza kuzungumza na kukaa chini. Mwanasheria wa makapuni yote naye akasimama.

“Kama alivyo tangulia kuzungumza mwenzangu, hata kwa upande wangu huku nami niliweza kuachiwa fomu ya urithi inayo muonyesha Ethan Klopp ndio mrithi wa kila mali ya mzee. Asanteni”

Mwanasheria huyo mara baada ya kuzungumza hivyo akakaa chini na kuwafanya wazee hawa hususani aliye kuwa muongeaji sana kukaa kimya huku akiwa mnyonge kabisa.

“Nimewaita hapa kutoka nahitaji kuwapa taarifa mbaya.”

Wazee wote wakanitolea macho wakionekana kustuka.

“Dada Mery naomba ukamuite dokta Alfonce”

“Sawa”

Dada Mery akasimama na kupandisha gorofani, baada ya dakika kama mbili havi wakarudi huku wakiwa wameongozana na daktari. Daktari Alfonce akawasalimia viongozi hawa”

“Naomba uje hapa dokta”

Nilizungumza kwa ukakamavu hadi mimi mwenyewe nikajishangaa, kwa umri wangu huu, inakuwaje ninakuwa jasiri sana.

“Dokta naomba uzungumze nao kile kinacho endelea”

“Asante Ethan”

Daktari akakohoa kidogo kisha akanitazama usoni mwangu, kwa ishara ya macho nikamuomba aweze kuzungumza kile ambacho kinaendelea.

“Mzee Joradan Klopp amefariki dunia”

Watu wote humu ndani wakastuka huku wakinitazama usoni mwangu.

“Mzee Klopp alikuwa akisumbuliwa na saratani ya damu, amefariki jioni hii. Mukiwa kama watu wa karibu kabisa na hii familia tumeona ni vyema tuweze kuwapa taarifa awali kabisa kanbla taarifa hii haijatoka kwenye vyombo vya habari. Yangu ni hayo”

Baada ya daktari kuzungumza hivyo akaka kwenye sofa.

“Taarifa hii ni nzito kwa kila mmoja wetu. Tunacho hitaji ni ushirikiano wenu. Kwa upande wangu nimemaliza. Dada Mery una lolote la kuzungumza?”

Dada Mery akatingisha kichwa akimaanisha kwamba hana chochote cha kuzungumza.

“Daktaria ninaomba uandae utaratibu wa watu kwenda kumuona mzee kabla hatujakwenda kumuhifadhi hospitalini mwili wake”

“Sawa”

Nilipo maliza kuzungumza nikatoka nje ya nyumba hii. Nikaelekea kwenye moja ya bustani na kuanza kulia kwa uchungu sana kwa maana nimepewa jukumu moja zito nikiwa bado nina umri mdogo sana.

“Ethan”

Niliisikia sauti ya dada Mery nyuma yangu, nikegeuka na kumtazama.

“Ethan nahitaji kuzungumza na wewe kama itawezekana”

Nikajifuta machozi kisha nimkubalia kwa kutingisha kichwa.

“Pole kwa majukumu ambayo baba amekubebesha, natambua swala zima la kusimamia mali zake ni jambo gumu na zito na isitoshe kwamba una umri mdogo”

“Asante, ila dada wewe ndio msaada wangu mkubwa sana kwenye hili swala. Peke yangu siwezi, peke yangu nahisi nitashindwa”

Nilizungumza huku machozi yakitumwagika sote wawili. Tukakumbatiana kwa nguvu huku, baada ya muda kidogo tukaachiana mara baada ya kumuona mwanasheria wa familia akitufwata hapa tulipo simama.

“Samahani kwa kuwasumbua”

“Bila samahani”

“Je ninaweza kuwaita waandishi wa habari ili waweze kuitoa taarifa hii”

“Ndio”

“Sawa sawa”

Mwanasheria akaondoka na kutuacha wenyewe.

“Ethan kuna mtu unapaswa kumpa habari kabla ya yeye kuweza kuisikia kwenye vyombo vya habari”

“Nani?”

“Camila”

“Naomba unisaidie simu yako”

Nilizungumza kwa unyonge.

“Sijui hata nimeiacha wapi”

“Ngoja nikatumie simu ya ndani”

Nikaelekea ndani, nikachukua simu ya sebleni na kupiga namba ya shuleni kwa Camila. Simu yake ikapolewa na sekretari wa shule hiyo, nikajitambulisha na kutokana si mara yangu ya kwanza kupiga simu, nikakubaliwa kuongea na Camila na nikaombwa nisubiri kidogo ili aweze kwenda kuitwa.

“Ethan mama ameamka”

Daktari alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.

“Sawa nina kuja kumuona”

“Sawa”

“Ethan”

Niliisikia sauti ya Camila akizungumza kwa furaha.

“Mambo”

“Poa mpenzi wangu, mbona unazungumza kwa unyonge hivyo kuna tatizo?”

“Ndio mpenzi wangu”

“Tatizo gani tena mpenzi wangu?”

“Baba amefariki”

“Nini!!?”

Camila aliniuliza kwa mstuko mkubwa sana.

“Ndio amefariki kama lisaa moja na nusu hivi “

“Ohoo Mungu wangu”

Camila alianza kulia taratibu.

“Amekufaje?”

“Ninakuomba uzungumze na mama na chukuru ruhusa uje huku”

“Sawa mume wangu, ninakuja sasa hivi”

“Sawa”

Nikakata simu, nikirudisha sehemu nilipo itoa kisha nikaelekea chumbani, nikamkuta bibi Jane Klopp akiwa amekaa pembeni ya mwili wa mume wake huku akiendelea kulia. Taratibu nikamsogelea na kulaza kichwa chake kwenye bega langu.

“Mama”

“Ethan bora ningeenda na mume wangu, kwa nini ameniacha peke yangu ehee?”

Mama alizungumza kwa uchungu sana, sikuwa na jinsi zaidi ya kuendelea kumbembeleza. Mwanasheria akasimama mlangoni na kwa ishara akaniita.

“Mama nina kuja”

“Sawa”

Nikamuachia mama na nikamfwata mwanasheria wa familia.

“Waandishi wa habari wamesha fika”

“Umewaandalia sehemu ya kuzungumza nao”

“Ndio”

“Ninakuja”

“Sawa sawa”

Nikarudi sehemu alipo mama. Nikamshika mikono yake huku nikimtazama usoni mwake.

“Mama”

“Mmmm”

“Ninakwenda kuzungumza na waandishi wa habari”

“Sawa naomba ujikaze mwanangu”

“Sawa mama”

Nikamtazama daktari aliye kaa kwenbye moja ya sofa humu ndani.

“Nakuomba umtazame mama”

“Sawa sawa”

Nikatoka ndani humu na kuongozana na mwana sheria hadi kwenye moja ya bustani. Nikawakuta wana habari wengi wakiwa wamekusanyika huku wakiwa wamebeba kamera za kurekodi na kupiga picha za kila tukio ambalo linaendelea katika eneo hili. Nikamuona dada Mery akiwa amesimama mbali kidogo na hapa tulipo, nikamfwata na kusimama naye.

“Unahitaji kuonekana na wewe kwenye hii taarifa”

“Hapana Ethan nina shindwa kufanya hivyo”

“Kwa nini?”

“Nenda tu Ethan”

Dada Mery alizungumza huku machozi yakimtiririka usoni mwake. Nikaruidi eneo walipo waandishi wa habari na kusimama katika sehemu niliyoa ndaliwa kusimama. Nikawatazama waandishi hawa wa habari, nikatazama saa yangu ya mkononi na kuona ina nionyesha sasa hivi ni saa moja usiku.

“Habari zenu”

“Salama”

“Kwa wale wasio nifahamu ninaitwa Ethan Klopp. Nina habari ambayo sio nzuri kwa familia na hata wapenzi wa soka”

Nilizungumza huku machozi yakinilenga lenga usoni mwangu.

“Masaa mawili yaliyo pita, baba yetu mzee Klopp ametutoka duniani”

Waandishi wa habari nao wakaonekana kustuka kidogo huku kila mmoja akiweka sawa kamera yake.

“Nilikuwa shule, nikarudishwa nyumba, ila kwa bahati mbaya nilimkuta mzee akiwa katika hatua za mwisho kabsisa za maisha yake”

Nikakaa kimya huku nikijifuta machozi usoni mwangu. Waandishi wa habari wakaanza kunyoosha mikono juu ili kunihoji maswali, ila nikashindwa kumjibu yoyote kwani hali ninayo isikia sio nzuri kabisa. Nikaondoka na kumuacha mwanasheria wa familia akizungumza. Nikaingia ndani. Daktari akainiita kwa ishara na nikamfwata pale alipo.

“Ndio”

“Mwili wa marehemu unatakiwa kwenda kuhifadhiwa sasa, sindano tuliyo mchoma nguvu yake itaisha mara baada ya muda mchache kuanzia hivi sasa”

“Sawa gari la wagonjwa si lipo tayari?”

“Ndio hata gari za polisi zimesha fika katika eneo hili”

“Sawa munaweza kuupeleka tu hospitali”

Maandalizia ya kuutoa mwili wa mzee Klopp yaakaanza kufanyika, huku kwenye televishion taarifa zinazo samba zinahusiana na kifo cha mzee Klopp, ikiwa ni pigo kubwa kwa taifa la Ujerumani hususani kwenye tathini ya michezo, kwani mzee Klopp aliichezea timu ya taifa ya nchi hii miaka kadhaa ya nyuma iliyo pita. Waziri mkuu akatangaza msiba huu ni msiba wa taifa, na bendera ya taifa ikashushwa nusu mlingoti. Camila na mama yake wakafika nyumbani hapa majira ya saa tatu usiku. Camila moja kwa moja akanifwata na kunikumbatia kwa nguvu huku akimwagikwa na mchozi usoni mwake.

“Kweli baba amekufa?”

“Ndio”

“Ethan pole sana mwanangu”

Mama Camila alizungumza huku akitukumbatia wote wawili.

“Asante sana mama”

Nilizungumza huku nikiendelea kulia kwa uchungu. Watu washuhuri na wafanya biashara kutoka maeneo mbali mbali wakafika katika jumba hili la mzee Ethan na ulinzi ukazidi kuimarishwa.

‘Ethan’

Niliisikia sauti ya Ethan mwenzangu katika ufahamu wangu wa akili.

‘Vipi?’

Nilimjibu kimoyo moyo pasipo watu wengine kuweza kufahamu ni nini ninacho kizungumza.

‘Kuna watu wana mpango wa kukuua usiku huu, kuwa makini la sivyo jua la asubuhi huto weza kuliona’

Maneno ya Ethan yakanistua sana kwani watu walio fika nyumbani hapa ni wengi sana hadi sujui nani ni mzuri au nani ni mbaya, jambo lililo anza kunipa wasiwasi moyoni mwangu.



‘Mungu wangu, ni kina nani hao Ethan’

Niliuliza huku nikiendelea kutazama watu waliomo katika eneo hili.

‘Kuna mameneja sita wamejiunga ili kuhakikisha kwamba wanakuangamiza na mali zote zinakuwa chini yako’

‘Nionyeshe basi Ethan niweze kuwajua’

Niliendelea kuzungumza huku wasiwasi ukizidi kunitawala moyoni mwangu.

‘Ethan dada yako ametekwa’

Sauti ya Ethan ikanistua sana na kujikuta nikianza kukimbia kuelekea chumbani kwake, nikaingia na sikumkuta.

‘Ametekwa wapi?’

Nilimuuliza Ethan mwenzangu ila hakunijibu chochote.

‘Niambie basi’

‘Chungulia dirishani’

Kwa haraka nikakimbilia dirishani na kuona gari aina ya BWM X5 ikitoka getini.

‘Wale ndio watekaji, wanaondoka’

Niliisikia sauti ya Ethan huku nikishuhudia jinsi gari hilo linavyo tokemea kwenye upeo wa macho yangu. Kabla sijatoka ndani humu mlio wa simu ya mezani katika chumba hichi ukanistua sana. Nikaitazama kwa muda huku jasho likinimwagika usoni mwangu.

“Ethan”

Sauti ya Camila ikanifanya nimtazame mlangoni alipo simama.

“Yaaa”

“Kuna mzee anahitaji kuzungumza na wewe huku chini”

“Ninakuja”

Camila akanitazama kwa unyonge kisha akatoka chumbani humu, nikaichukua simu hii na kuipokea na kuiweka sikioni mwangu.

“Haloo”

“Hatuna muda wa kukuelezea, tunacho hitaji ni kufanya mabadilishano. Tunahitaji uweze kuwaambia wana sheria wako wabadilishe mali zote zitaandikwa kwa jina tunakalo kutajia la sivyo dada yako anakwenda kufa umenielewa”

“Yupo wapi dada yangu”

“Ethan usifa…..”

Niliisikia sauti ya dada Mery akizungumza huku akilia kwa nguvu sana.

“Naamini kwamba ume msikia”

“Munacho hitaji ni mali tu si ndio”

“Ndio”

“Mumezipata, niambieni ni wapi na saa ngapi niwapatie mali hizi”

Usikae mbali na simu, tutakufahamisha na ole wao uweze kumueleza mtu wa aina yoyote juu ya hili tuta kuua”

“Nimekuelewa”

Nilizunguza huku mwili wangu mzima ukinitetemeka kwa hasira, nikairudisha simu hii sehemu nilipo itoka kisha nikatoka ndani humu huku nikiwa nimevimba kwa hasira. Nikasimama katika ngazi za sebleni huku nikitazama watu hawa walio kusanyika huku wengine wakionekana wakiwa wameguswa sana na kifo cha mzee Klopp.

‘Ethan nahitaji kufanya kitu juu ya hili’

‘Kitu gani rafiki yangu’

‘Niambie ni nani na nani wanahusika katika mauaji utekaji wa dada yangu?’

‘Unamuona huyo mzee mwenye shati jeusi na shingoni ana kola nyeupe, na mkononi mwake amashika biblia?’

‘Ndio’

‘Huyo ni adui namba moja wa mzee wako na yeye ndio amekuja na hao vijana wakiwa kama mashemasi, ndio maana ili wawia urahisi kumteka Mery’

Nikaanza kushuka huku nikimkazia macho mzee huyu

‘Unataka kufanya nini, subiri sijamaliza maelezo ya swali ulilo niuliza’

‘Ethan nahitaji hadi kuna pambazuka hii kazi niwe nimesha imaliza’

‘Nimekuelwa rafiki yangu. Umemuona yule jamaa aliye bana nywele zake kwa nyuma?’

‘Ndio”

“Yule naye ni miongoni mwa wapangaji wa mpango huo. Sasa unaona wale mameja pale walio simama?’

‘Ndio’

Wale ndio wanatumikishwa na hao watu wawili nilio kuonyesha’

‘Ethan niwafanye nini?’

Nilizungumza huku machozi yakinimwagika usoni mwangu kwa hasira iliyo changanyikana na msiba mzito sana ambao nimeupata wa mzee huyu.

‘Waite wote na omba ukutane nao kwenye ofisi ya baba yako’

‘Sawa’

‘Ila usitumie hasira, kuwa mpole’

‘Sawa’

“Ethan”

Camila aliniuongelesha huku akinipa kitambaa cheupe.

“Nashukuru, muda ule ulisema nina itwa na nani?”

“Ni yule mzee mchungaji alihitaji kuzungumza na wewe”

Camila akanionyenyesha mchungaji huyo ambaye niliambiwa na Ethan.

“Sawa, kuna kikao kimoja nahitaji kufanya nao hawa watu, ila ninakuomba ukakae chumbani na mama yangu”

“Sawa, ila mama yangu yupo chumbani ana mfariji mama”

“Poa ila nakuomba ukakae naye”

“Sawa mpenzi wangu”

Camila akanibusu shavuni mwangu, kisha akapandisha ngazi za kuelekea gorofani. Nikaanza kutembea huku nikimtazama mchungaji huyo, ambaye baada ya kuniaona akatabasamu kwa bashaha.

“Ethan, tumsifu Yesu kristo”

“Milele amen askofu, samahani kwa kuchelewa kuitikia wito wako”

“Wala usijali mwanangu katika kristo, tunaweza tukapata muda na kuzungumza?”

“Sasa hivi”

“Ndio, ila ninakuomba tukazungumzie kwenye ofisi ya baba kule si unaifahamu”

“Yaa ninalifahamu lile lengo”

“Basi nakuomba utangulie ninakuja”

“Sawa mwanangu”

Mchungaji huyu akanibusu kwenye paji langu la uso, kisha akatoka sebleni hapa, huku nyuma yake akiongozana na mwanaume ambaye Ethan pia alinitajia. Nikaangaza angaza humu ndani, nikamuona mwanasheria wa makampuni akizungumza na mmoja wa mameneja. Nikamfwata na kumuomba nizungumze naye pembeni kwa sekunde.

“Ndio bosi”

“Kuna wageni wameelekea kule kwenye ofisi ya baba, ninakuomba ukake nao kwa muda kidogo mimi nina kuja na wageni wengine”

“Kuna kikoa mkuu?”

“Ndio, naokuomba unisaidie kuzungumza nao kwa muda”

“Sawa”

Mwanasheria akanielewa, kisha niwafwata hawa mameneja walio simama kikundi, walipo niona wakakatisha mada walio kuwa wakiizungumza huku dhairi inaonyesha kwamba ni mada ya siri, na mbaya zaidi yule meneja niliye msimamisha kazi masaa machache yaliyo pita naye ni miongoni mwao hawa wasaliti.

“Samahani wazee wangu, nathamini uwepo wenu na ninawashukuru sana. Tafadhali ninawaomba tukazungumze kitu kidogo kwenye ofisi ya baba”

“Sawa sawa mkuu”

“Mkuu hata mimi uliye nisimamisha kazi?”

“Ndio mzee wangu, hilo pia tutalizungumzi huko, unajua muda ule nilikuwa nina hasira na samahani kwa kukujibu vibaya na halikuwa lengo langu kufanya hivyo”

“Nashukuru sana muheshimiwa”

Mzee huyu alizungumza huku akitabasamu sana. Wakaanza kutoka ndani humu, nikashusha pumzi taratibu huku nikifikiria ni kitu gani ambacho ninakwenda kuzungumza nao.

“Ethan Klopp”

Dada mmoja aliniita huku akisimama mbele yangu

“Ndio”

“Mimi ni muandishi wa BBC hapa nchini Ujerumani, ninaweza kukuhoji maswali mawili matatu?”

“Naomba unipe kama nusu saa, nakuhidi nitakuja kwa ajili ya mahojiano yako”

“Sawa nashukuru”

“Karibu”

Nilijaribu kujikaza ili kuificha hasira yangu ambayo kusema kweli imenijaa kifuani mwangu. Nikaanza kutembea kuelekea katika jengo lenye ofisi ya mzee Klopp ambalo lipo mbali kidogo na jumba lake hili, ila vyote vipo katika eneo moja.

‘Ethan’

‘Ndio’

‘Ninakwenda kuzungumza nini?’

‘Kabla ya kuingia ofisi,nenda katika stoo’

‘Nikafanyaje’

‘Wewe nenda’

Nikabadilisha njia na kueleka katika stoo iliyopo katika jengo la ofisi.

‘Haya ninafanyaje sasa humu ndani’

‘Kuna bastola kwenye hiyo droo, ina risasi za kutosha na pembeni kuna kiwambo cha kuzuia risasi ifunge’

‘Weee unataka niende kuwaua?’

‘Sijasema uende kuwaua je wakitaka kukuua wewe utasemaje?’

‘Sawa’

Nikafungua droo, niliyo elekewa na Ethan na kweli nikakuta bastola, nikaichukua, kisha nikaichomeka nyuma ya kiuno changu na kufunika shati langu vizuri. Nikaona fimbo moja ya kuchezea mchezo wa gofu, nikaichukua huku nikiitazama vizuri, kisha taratibu nikaanza kutembea kuelekea katika ofisi ya baba.

“Mkuu niwewaweka katika ukumbi wa mkutano”

Mwanasheria aliniambia huku akinitazama mkononi mwangu.

“Naomba unisubiri hapa na hakikisha hakuna mtu ambaye anakuja humu ndani”

“Ila mkuu kazi yangu ni sheria na si ulinzi”

“Fanya hivyo kwa ajili yangu na kwa leo tu, haito jitokeza tena kwenye maisha yako sawa”

“Sawa mkuu”

Nikaondoka eneo hili na kumuacha mwanasheria akinishangaa sana. Nikafungua mlango wa ukumbi huu na kuwakuta watu wote wakiwa wamekaa huku wakiwa wameizunguka meza kubwa iliyopo humu ndani. Kila niliye muhitaji yupo ndani humu.

‘Funga mlango kwa code namba’

‘Sizifahamu’

‘Tisa ziwe tatu na ziro mbili na moja’

Nikaminya batani hizo kama Ethan alivyo niambia, nikatembea hadi kwenye kiti kilichopo mbele kabisa ya meza hiyo. Taratibu nikaa huku nikiatamana na watu hawa. Baadhi yao wanaonekana kujawa na dharua kubwa sana.

“Naamini sote tunafahamu ni kwa nini tupo hapa?”

“Wewe ndio umeitisha kikoa”

“Mwanangu katika kristo, mimi nilihitaji kuzungumza na wewe binafsi, ila si kwa kukaa na watu hawa”

“Mchungaji katika bwana tulia. Jamani mimi ni mdogo sana kwenu nina miaka hata kumi na nane sijafikisha. Jambo la kuachiwa makampuni makubwa ni kitu kilicho nistusha sana na kunichanganya kwa kweli”

“Nimeona niwaite wachache nyinyi ili niweze kuwasikia maoni yenu munasemaje juu ya mimi kuachia madaraka ya uangalizi wa kila kitu kwa mmoja wenu hmu ndani, au muna semaje?”

“Ni kweli mkuu ni maamuzi mazuri”

Meneja mmoja alizungumza huku akikenua meno yake kiasi cha kunifanya nitabasamu, ila moyoni nina ugulia kwa hasira kali sana.

“Ni kweli kiongozi ukituachia makampuni tunayo yaongoza na sisi tukawa tunakuletea asilimia, fulani labla kwa mwenzi hivi mambo yanaweza kuwa mazuri”

“Samahani wewe una simamia kampuni ya nini?”

“Mimi ninasimamia kampuni ya utengenezaji wa vifaa vya michezo, kama mipira, viatu, jezi na kadhalika”

“Wastan wa mwaka kampuni yako ina ingiza kiasi gani?”

“Dola zaidi ya bilioni nne”

“Nashukuru, siwezi kuwauliza wote kwa maana nitawapoteze muda. Ila nina jambo moja muhimu sana naamini mchungaji utanisaidia kwenye maombi”

“Zungumza tu mwanangu katika kristo”

“Ni nani aliye mteka dada yangu MERY?”

Watu wote wakastuka huku wakinitazama kwa umakini sana.

‘Ethan nafanyaje’

‘Ninakupa nguvu, hakuna atakeya kuweza’

Nikasimama kwa haraka huku nikihema mihemo mizito kana kwamba nicheza mpira kwa muda mrefu sana pasipo kupumzika.

“Nimewauliza?”

Nilizungumza huku nikiigonga meza hii na hii fimbo ya kuchezea mpira wa gofu. Mchungaji akatoa bastola yake na kuninyooshea.

“Dogo unahisi hii vita utaiweza kati yako na sisi. Baba yako aliweza kufanya ujinga ndio maana ametufikisha hapa tulipo. Tena muite mwanasheria wako aje hapa asainishe makubaliano ya kubadilisha mali zote na kuziingiza kwa majina tutakayo kuambia”

Nikamtazama mchungaji huyu, nikajikuta nikiruka mezani hapa hadi katika shemeu aliyo simama, kitendo hicho kikamuacha mdomo wazi. Nikamtandika konde zito la kifuani lililo mfanya arushwe mita kadhaa hadi ukutani na akaanguka chini. Mameneja walivyo ona hali imebadilika ndani ya chumba hichi wakanyanyuka na kutamani kukimbilia mlangoni, ila wakashindwa kutoka tayari nimesha ichomoa bastola yangu na kuwanyooshe.

“Anaye hitaji kufa akaguse ule mlango pale. Haya kila mmoja arudi kwenye kiti chake”

Mameneja wote wakarudi kwenye viti vyao na kukaa huku miili yao ikitetemeka.

“Kila mmoja aweke mikono yake juu ya meza”

Wote wakatii amri hadi mwanaume ambaye naye anahusika na mpango huu wa kumteka dada Mery na kuhitaji kuchukua mali kiurahisi. Nikaanza kuwapiga fimbo za mikono kwa kutumia fimbo hii ambayo imetengezwa kwa chuma. Mamenaja hawa wakazidi kulia kwa uchungu sana ila hapakuwa na hata mmoja wao ambaye alithubutu kufanya ujinga wa kunishambulia kwani kilicho tokea kwa mchungaji feki kila mmoja amekishuhudia, kwani ni jambo ambalo binadamu wa kawaida hawezi kulifanya na tukio kama hilo nahisi walisha liona kwenye baadhi ya filamu za Kimarekani kama Spider Men.



“Ni nani aliye mteka dada yangu”

“Ni yule kule mkuu”

Menjea mmoja alizungumza huku machozi yakimwagika kama mtoto mdogo. Nikamtazama mchungaji aliye mnyooshea mkono, kwa haraka nikamfwata mchungaji huyu na kumnyanyua kwa mkono mmoja hadi wote wakashangaa, kwani kwa umri wangu, sina nguvu ya kunyanyua mwanaume kama huyu.

Nikamkalisha mchungaji juu ya kiti chake huku akionekana kuona mawenge mawenge. Nikaanza kumpapasa kwenye suruali yaka na nikatoa simu, nikaiweka mezani huku nikimtazama usoni mwake.

“Wapigie vijana wako wamrudishe dada yangu ndani ya dakika kumi, la sivyo nitavuja kichwa chako na weka loud speaker”

Mchungaji huku akitetemeka mwili mzima, akaichukua simu yake na kuanza kuiminya minya. Akataka kuiweka sikioni mwake, ila kwa ishara nikamuamrisha kuiweka mezani, ila hata anacho kizungumza watu wote waweze kukielewa.

“Ndio boss”

“Mark mrudisheni huyo binti sasa hivi”

“Boss”

“Nimesema mrudisheni sasa hivi sihitaji maswali pumbavu wewe”

“Nahitaji kungumza na Mery nijue yupo salama”

“Wewe ni nani?”

“Acha kuuliza, fanya ulicho ulizwa”

“Ethan”

“Ndio dada yangu upo salama”

“Ndio, ila naona wanageuza gari sijui wanaelekea wapi?”

“Wanakurudisha nyumbani, ikitokea mtu akakushika hata ziwa lako niambie itamgarimu”

“Sawa Ethan”

Nikaichukua simu hiyo na kuikata, kisha nikaibwaga mezani.

“Kuna jambo moja nahitaji niliweke wazi kwenu. Mimi sio mjinga na musijidanganye mukahisi mali hizi nilizo achiwa siwezi kuziongoza, ninaweza tena mara kumi ya hata sasa hivi kwa maana mzee alisha niandaa kuwa kiongozi toka nikiwa nia miaka saba, sijui tunaelewana”

“Ndio Boss”

Waliitikiwa kwa unyonge huku wengine wakijipangusa macho kwenye mashavu yao.

“Leo nitawaandishika mkataba wa kifo.”

Wote macho yakawatoka huku wakinitazama kwa umakini.

“Mkataba huu, yoyote atakaye kiuka masharti, basi kama mkataba unavyo sema. Basi adhabu yake ni kifo cha aina yoyote ambacho siku hiyo nitaamua kumpatia sijui tumeelewana?”

“Ndio mkuu”

Waliitikia huku wakilia kwa uchungu sana. Nikafungua mlango wa kutokea ukumbinu humu, nikamuita mwanasheria kwa iashara.

“Ndio”

“Unaweza kuniandalia mikataba muhimu”

“Sasa hivi?”

“Ndio”

“Ngoja nikachukue laptop”

“Fanya hivyo”

Mwanasheria akaondoka kisha nami nikarudi kwenye kiti changu.

“Haya yaliyo tokea humu, endapo nitayasikia nje ya hapa basi sinto muacha hata mmoja wenu hai, sinto jali ni wewe, au wewe, au wewe ambaye ulitoa siri. Akifa samaki mmoja basi ni wote wanakufa”

Maneno yangu yakazidi kuwaogopesha mameneja hawa, baada ya muda mwanasheria akarudi huku akiwa ameongozana na dada yangu Mery.

Wote wakaonekanekana kujawa na mshangao kwa maana watu waliomo humu ndani sura zao zimejawa na huzuni kubwa kuliko hata sisi wenye msiba wetu. Nikanyanyuka na kumfwata Mery sehemu alipo simama, nikakumkumbatia kwa nguvu huku kichwa chake akikilza begani mwangu.

“Pole saana dada yangu”

Nilizungumze huku nikiendelea kumkumbatia kwa nguvu.

“Asante. Ethan ni nini kinacho endelea?”

“Tutuzungumza baade, naomba ukakae chumbani pamoja na mama”

“Ethan naogopa”

“Usijali dada yangu, kila kitu kitakwend vizuri, sawa”

“Sawa, alafu yule mchungaji pale ndio mwenye vijana wake walio niteka”

Dada Mery alizungumza kwa sauti ya kuninong’oneza huku akinitazama usoni mwangu.

“Usijali nitalishuhulikia, wewe fanya kama nilivyo kuambia dada yangu”

“Sawa, ila inabidi tuwafahamishe askari kwa maana yule mchungaji sio mtu mzuri kabisa”

“Hakuna haja”

“Kwa nini?”

“Kila kitu niachie mimi”

Dada Mery akanikazia macho huku aki akinitazama usoni mwangu.

“Sawa”

Dada Mery akamtazama mchungaji kwa jicho kali kisha akatoka ndani humu, nikaufunga mlango kwa ndani na kurudi kwenye kiti changu nilicho kuwa nimekaa.

“Samahani mwana sheria kwa kukusumbua”

“Bila samahani mkuu”

“Nahitaji uandike mkata utao sainiwa na kila mtu humu ndani ya hichi chumba. Mkataba huo ni wa mwaka mmoja katika kuiongoza kampuni anayo iongoza. Masharti ya mkabata huo, nahitaji hadi inafika tarehe ya kama leo na mwezi kama wa leo, mwaka ujao, kila mmoja kwenye kampuni yake awe ameingiza mapato mara mbili ya mapato anayo ingiza hivi sasa hivi. Kwa yoyote atakaye shindwa, adhabu yake ni KIFO”

Mwanasheria macho yakamtoka huku akionekana ni jambo jipya kwa yeye kulisikia.

“Ethan pasipo kukuvunjia heshima, ila hili swala halipo katika sheria yoyote hapa nchini Ujerumani”

Mwanasheria alizungumza huku akinitazama, mameneja wote pamoja na mchungaji na mwezake wamekaa kimya kwani wanatambua ni kitu gani nilicho wafanya.

“Hiyo ni sheria yangu na mali zangu. Unatambu kwamba huyo mchungaji leo alihitaji kuniua na ndio aliye mteka Mery”

“Mery alitekwa….!!?”

“Ndio na mchungaji ndio mtekaji, huyo jamaa mwenye manywele yake, naye ni mshawishi kwa hawa wajinga sita hapa ili kila mmoja ajimilikishe kampuni anayo iongoza.”

Maneno yangu yakazidi kumshangaza mwana sheria pamoja na hawa watu wengine kwa maana nina hisi kitu wanacho jiuliza sana, nimejuaje juu ya mipango yao ya siri.

“Ninajua kila mpango wenu na ninajua munacho kifikiria juu ya kutoka hapa. Sasa ole wake mtu yoyote afanye ubadhilifu hawa wa dola moja ndani ya kampuni, mkataba wako utaisha siku ambayo utaonana na mimi nikiwa katika sura nyingine”

“Kwa aliye iba pesa za kampuni na kuhamishia pesa Uingereza, Uswiz, na sehemu nyingine duniani. Nahitaji hadi inatimia saa moja asubuhi pesa muwe mumezirudisha kwenye akaunti za viwanda.”

Baada ya kumaliza kuwapa mameneja maagizo yangu, nikamgeukia mchungaji na mwenzake.

“Wewe una jishuhulisha na kitu gani?”

“Ni…ni ni muuzaji wa magari kwa nchi za Asia na Afrika”

“Nahitaji asilimia sabini ya hisa zako za kampuni yako kabla ya saa moja asubuhi, ila kama huitaji nilicho mfanya mchungaji ni mara mbili na kile nitakacho kufanya wewe”

“Asilimia sabini?”

“Ndio au nimezungumza kilugha.”

“Samahani mkuu”

“Mchungaji una miliki nini, ole wako unidanganye?”

“Nina kasino moja lipo Munich, nina hotel ipo London na nina kanisa lina matawi mia moja na hamsini ndani na nje ya Ujerumani”

“Nahitaji asilimia sabini ya kipato kitokanacho na makanisa yako yote kingie katika mashirika ya kusaidia watoto yatima barani Afrika hususani Tanzania”

“Sawa mkuu”

“Tena, mwanasheria utanisaidia kufungua shirika ambalo nitaliita Ethna Childrean Foundation”

“Sawa sawa”

“Pesa yote ingiza kwenye shirika nitakalo lifungua, sijui umenielewa?”

“Nimekuelewa mkuu”

“Mwanasheria kufungua shirika inachukua muda gani?”

“Kama wiki hivi mkuu, kwani tutafwata sheria zote za kiserika na kutokana ni shirika ambalo ni la msaada kwa mataifa yote duniani, ndio maana litachukua muda hivyo”

“Nashukuru”

Nikajilaza vizuri kwenye kiti changu hichi cha kuzunguka huku nikiwatazama watu wote humu ndani.

‘Hii ndio nguvu niliyo kuwa nikikueleza toka ulivyo kuwa mtoto’

‘Kweli nime iona hiyo nguvu’

‘Kwa umri wako ila wana kuogopa kuliko hata simba’

‘Hivi kweli hawato nisaliti?’

‘Kwa sasa hakuna ambaye ata kusaliti. Wameshika adabu yao’

‘Hahaaa, ila nashukuru sana msaada wako’

Nilizungumza kimoyo moyo na hakuna hata mmoja ambaye anasikia mazungumzao yangu mimi na Ethan’

‘Usijali ni jukumu langu na niliweka ahadi toka usiku ule ulivyo weza kutupwa mtoni’

‘Ehee nimekumbuka’

‘Umekumbuka nini?’

‘Ni kina nani walio nitupa mtoni na ilikuwaje?’

‘Usijali, nitakuelea kila jambo pale nitakapo pata muda’

‘Leo huwezi nieleza?’

‘Maliza kwanza kitu kimoja, ndio ufwate jambo jengine.’

‘Sawa sawa’

“Nimemaliza mkuu”

Mwanasheria alizungumza huku akinyanyuka kweye kiti chake. Akabeba laptop yake hadi kwenye mashine ya kutolea kopi, akatoa kopi ya karatasi kadhaa kisha akaanza kuzitandaza mezani kwa kila mmoja. Akanikabidhi na mimi karatasi moja. Nikaisoma, kila nilicho muhitaji aandike amekifanya kama vile ninavyo hitaji.

“Mikataba yetu, inaeleweka na inasomeka vizuri na muna saini tukiwa na mwana sheria wa kampuni zote. Haya sasa kazi kwenu, muna kalamu au tuwa azime”

“Mimi ninayo”

 ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

BLOG