Search This Blog

Wednesday, November 18, 2020

POWER SEHEMU YA 6/10

 

 


 POWER

WRITER…………………………………………EDDAZARIA G.MSULWA
WEBSITE………………………………………… www.storyzaeddytz.com
CONTACT……………………………………….. 0657072588/0768516188
AGE……………..18+ 

SEHEMU YA 6 KATI YA 10

 


“Ndio na ili awe na maisha marefu katika kuiongoza hii nchi kwa awamu zote mbili. Mlinzi wa pekee ni wewe na ili atomize hayo nilazima uweze kufanya maamuzi magumu sana ambayo kwa namna moja ama nyingine lazima yakutengenezee maadui wengi sana”

“Maamuzi gani?”

Ethan akanitazama kwa sekunde kadhaa.

“Lazima uweze kuachana na Camila pamoja na Biyanka na kama haitoshi inabidi huyu binti Qeen uweze kumuua kwani endapo ataungana na maadui zako kutokana na ujinga wake tu wa wivu ujue baba utazidi kuwa katika hali ngumu sana ya kimaisha kwani huu mchazo wote mulio ufanya ana ufahamu”

Maneno ya Ethan taratibu yakanifanya nianze kupunguza mwendo wa gari langu na kulisiamamisha pembeni ya barabara huku nikiwa na wasiwasi mwingi sana.

“Hiyo ndio njia ya pekee ya wewe kumfanya mwana mama huyu kuwa madarakani. La sivyo ndani ya miaka miwili yake ya uongozi ni lazima aweze kuuwawa, kwani wapo watu nyuma hawahitaji nchi hii uiongozwe na mwanamke, kwani hata raisi mwanamke wa miaka hiyo ya nyuma aliye kuwa akiingoza hii nchi aliwawa kikatili na Dany tena kwa kukatwa kichwa chake”

“Heee?”

“Ndio kipindi hicho wewe bado ulikuwa hujazaliwa”

“Raisi huyo aliitwa nani?”

“K2, ukifwatilia historia yake utaweza kuifahamu vizuri”

“Sasa nikiachana na Camila pamoja na Biyanka. Sasa mimi nitaishije?”

“Leo kwani umemuona nani?”

“Hawa”

“Basi halali yako”

Ethan akapotea kwenye uwepo wa macho yangu na kunifanya niweze kujawa na maswali mengi sana kichwani mwangu. Nikawasha gari na kuendelea na safari yangu. Majira ya saa kumi na mbili jioni nikafika nyumbani kwa mzee Poul Mkumbo huku nikiwa nimechoka sana na njaa kali ikiwa imenikamata kisawa sawa. Nikaingia ndani na kukutana na Biyanka sebleni, kwa haraka akanikimbilia na kunikumbatia kwa nguvu, tukanyonyana lispi zetu huku moyoni mwangu nikifikiria siku ya kumuacha binti huyu sijui atakuwaje.

“Mama anaendeleaje?”

“Yupo vizuri japo si sana.”

“Baba yupo?”

“Ndio”

Nikamuomba Biyanka akaniitie mzee Poul Mkumbo. Akaniachia na kuelekea chumbani kwa wazazi wake, baada ya dakika kadhaa wakafika sebleni hapa, ndani ya masaa kadhaa mzee huyu amepungua mwili wake, yote ni kutokana na mawazo. Nikasalimiana naye kisha nikamkabidhi faili hili, taratibu akaanza kulifunua, uso wake ukaanza kujawa na tabasamu alipo maliza kulisoma faili hili, akanipa mkono wake wa kiume, taratibu nikaupokea na akautingisha mkono wangu kwa furaha kubwa sana.

“Safi sana mkwe wangu. Sasa na yeye lazima akose uraisi. Pumbavu sana”

Mzee Poul Mkumbo alizungumza huku matumaini ya kumuharibia mpinzani wake yakimjaa jambo ambalo likikamilika nina imani bi Tasiana Ramadhani anakwenda kuwa raisi wa nchi hii na yale yote niliyo kubaliana naye yanakwenda kutimia kwa asilimia mia moja.



“Ethan ni nini?”

Biyanka aliniuliza huku naye akiwa na shahuku kubwa ya kuhitaji kuweza kufahamu ni kitu gani kinacho endelea kati yangu mimi na baba yake.

“Ni ushiahidi unao onyesha kwamba mgombea uraisi wa chama pinzani, kwanza si raisi wa Tanzania pili kuna matukio ameyafanya ya kunajisi watoto wa kiume”

“Weeee!!”

Biyanka alizungumza huku akiwa amejawa na mshangao mkubwa sana. Kwaharaka akamsogelea baba yake na kuchukua faili hilo, akaanza kulipitia kurasa moja baada ya nyingine.

“Baba hii inatosha kabisa kuhakiksiha kwamba unatoa siri za mzee huyu hadharani”

“Yaa ila kuna sehemu nitahakikisha kwamba nina mbana”

“Sehemu gani baba?”

“Ninajua mimi. Mkwe asante sana nitaendelea kukupenda na kukuamini kwa maana unapambana juu ya hii familia tofauti kabisa na ninavyo fikiria”

“Nashukuru sana baba mkwe”

Mzee Poul Mkumbo akachukua faili hilo kutoka mikononi mwa Biyanka kisha akaondoka sebleni hapa. Biyanka akanikumbatia kwa furaha kwa maana si baba yake tu atakuwa amepoteza nafasi ya kuwa raisi katika nchi hii, ila hata mpinzani wake namba moja naye hato weza kuwa raisi wa nchi hii. Biyanka akaniandalia chakula mezani, na taratibu tukaanza kula kwa pamoja.

“Mume wangu kwa nini unafanya haya yote ikiwa sisi tulisha kata tamaa”

Biyanka aliniuliza kwa sauti ya upole na iliyo jaa hisia za kimahaba.

“Mimi sio mtu wa kukata tamaa kirasi mpenzi wangu. Unajua ningekuwa ni mtu wa kukata tamaa basi leo hii nisinge kuwepo hapa”

“Kusema kweli ninazidi kukupenda kila siku. Yaani umempa baba yangu matumaini mapya kwani adui yake naye anakwenda kuanguka”

“Ni kweli, ni bora wakose wote. Hata akija mwengine kidogo chama chake kitakuwa hakina nguvu na msimu mwengine baba akijipanga vizuri zaidi ya hapa basi anachukua nchi”

“Kweli mume wangu unaona mbali sana kwa kweli”

“Yaa hii ni siasa mpenzi wangu”

Tukamaliza kupata chakula hichi cha usiku. Tukaingia chumbani, Biyanka akaanza kunivua nguo zangu taratibu na nilipo baki na boksa, akaingiza kiganja chake eneo la jogoo wangu.

“Nimemiss mpenzi wangu”

“Kweli?”

“Ndio nina hamu naye tena sana”

Biyanka taratibu akanivua boksa yangu huku taratibu akichuchumaa. Taratibu akaanza kumnyonya jogoo wangu huku mikono yangu yote miwili ikishika kichwa chake. Msisimko wa kimahaba ukazidi kuongezeka kwetu sote wawili, nikamnyanyua Biyanka na kumlza kitandani, nikamvua sketi yake hii fupi aliyo ivaa, nikafungua mikanda ya bikini yake kisha taratibu nikaanza kula utamu wa tunda lake. Mtanange huu ukadumu zaidi ya nusu saa na wote kwa pamoja tukajikuta tukifikia tamati kwa pamoja huku kila mmoja akionekana kujawa na raha pamoja na furaha kubwa sana moyoni mwake.

***

Siku ya kutangazwa matokeo ikafika. Watanzani wengi kila mmoja ana hamu ya kuweza kusikia ni nani ambaye anaweza kushinda kiti cha uraisi huku wengi wao wakiwa na imani kubwa sana mgombea wa chama pinzani kwamba ni lazima aweze kushinda matokeo haya. Siku hii sikuhitaji kukaa nyumbani kwa mzee Poul Mkombo na moja kwa moja nikaelekea kazini kwangu. Nikajumuika na wafanyakazi wangu katika ukumbi wa kusubiria wa kampuni yangu na kila mmoja macho yake yapo katika tv kubwa sana iliyopo ndani ya ukumbi huu. Meseji fupi ikaingia kwenye simu yangu.

‘Yaani nina presha mwanagu’

Nikatabasamu kidogo kwani meseji hii imetoka kwa bi Tasiana Ramadhani.

‘Usijali mama yangu’

‘Mmmm haya ila kweli nitafanikiwa mwanangu’

‘Mama wewe jiamini’

‘Sawa baba’

“Mkurugenzi karata yako unaitupia wapi.”

Mmoja wa wafanyakazi wangu niliye kaa naye pembeni aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.

“Mmmm karata yangu kwa kweli haipo kwa kiongozi yoyote.”

“Kwa nini mkurugenzi?”

“Kura yangu ilikuwa ipo kwa baba yangu mkwe ila ndio hivyo alijiuzuru”

“Yaa kweli, ila samahani mkuu naweza kukuuliza swali?”

“Uliza tu swali?”

“Kwa nini baba yako mkwe aliamua kujitoa kwenye kinyang’anyiro?”

“Mmm ni stori ndefu kidogo, ila sababu alizo zitaja kwenye vyombo vya habari ndio sababu husika zilizo mpelekea kujitoa”

“Mmmmm ila alikuwa na nafasi ya kuchukua kabisa uraisi”

“Ni kweli nafasi alikuwa nayo ila mambo ndio hivyo jinsi yalivyo tokea”

“Sawa muheshimiwa”

Saa ya kutangaza matokeo ikawadia. Ukumbi mzima ukaa kimya huku wote tukimtazama kiongozi mkuu wa tume ya uchaguzi akitangaza matokeo hayo. Akaanza kutangaza idadi ya wapiga kura, akatangaza kura zilizo pigwa na zilizo haribika.

“Mshindi wetu aliye jipatia kura nyingi ni bibi Tasiana Ramadhani”

Baadhi ya wana mama waliomo humu ukumbini wakaanza kupiga makofi huku watu wengi wakionekana kama kuto kuamini kile kilicho tokea. Mchukua video akaisogeza karibu sura ya mgombea wa chama pinzani ambaye uso wake naye umeonekana kujawa na mshangao. Nikamshuhudia bi Tasiana Ramadhani akinyanyuka kwenye kiti alicho kikalia na kushangilia huku wapambe wake wake kadhaa alio ambatana nao wakiungana naye katika kushangulia sana. Moyoni mwangu nikajawa na furaha kubwa sana kwani mpango wangu umekwenda kama vile nilivyo tegemea. Nikanyanyuka na kutoka ukumbini humu, nikaelekea ofisini kwangu na kutoa simu yangu nikampigia Roman.

“Ndio bosi”

“Kazi nzuri”

“Nashukuru sana bosi.”

“Upo na hao mabibie?”

“Ndio nipo nao hapa”

“Basi waambie wasiondoke ninakuja”

”Sawa mkuu”

Nikakata simu, kabla sijairudisha mfukoni mwangu simu yangu ikaita, nikaitazama vizuri na kukuta ninamba ya Hawa, nikaitazama kwa sekunde kadhaa kisha nikaipokea.

“Ndio”

“Ohoo asante sana Ethan, sikutarajia kabisa kwenye maisha yangu kama hili jambo linaweza kuwa hivi”

“Usijali, kikubwa ni kuwa makini na kufunga vinywa vyenu”

“Usijali katika hilo, yaani sijui mama atajisikiaje kwa kweli”

“Nilichati naye muda fulani. Nina imani kwamba yupo kwenye hali nzuri hivi sasa”

“Kweli, ngoja tukitoka hapa ukumbiti tutakupigia”

“Sawa”

Nikakata simu na kutoka nje, nikaingia kwenye gari yangu na kuelekea moja kwa moja hadi maeneo ya Mbezi Beach anapo ishi Roman, nikapiga honi na geti likafunguliwa na nikaingia ndani. Qeen akanipokea kwa furaha kubwa sana huku akinikumbatia na kunipiga mabufu mengi mdomoni mwangu.

“Tumefanikiwa Ethan”

“Yaa mpango umekwenda vile tulivyo panga mpenzi”

“Siamini jamani chama tawala tumekiangusha”

“Ndio hivyo kila jambo ni muda ya tageti”

Tukaingia ndani na kumkuta Latifa akiserebuka mziki kwa furaha kubwa sana ambayo hakika imetawala kwa kila mmoja wetu.

“Mimi ni mtu wa kuweka ahadi na siwezi kuiangusha ahadi yangu kwenu. Kila mmoja leo hii namuingizi kiasi cha pesa nilicho muahidi hapa hapa”

“Weee”

“Ndio au amuniamini?”

“Tunakuamini mkuu”

“Ila hizi pesa inabidi muweze kuziingiza kwenye account ambayo sihitaji muweze kuhisiwa vibaya hata ikitokea kumefanywa uchunguzi na taasisi za kufanya uchunguzi kama takukuru.”

“Kama ni hivyo mkurugenzi inabidi utupe muda kidogo wa sisi kuweza kufungua account nje ya nchi”

“Sawa. Ila Roman nahisi wewe unayo accont?”

“Ndio mkuu ninazo accont nyingi tu”

Nikaanza kufwata hatua za kuhamisha pesa kutoka kwenye accont yangu na kuingiza kwenye accont ya Roman iliyopo nchini Uingereza.

“Nashukuru mkuu nimeipata”

“Hembu Roman nione umeingiziwa kiasi gani?”

Latifa alizungumza huku akitaka kutazama simu ya Roman aliyo ishika mkononi mwake.

“Mmmmm kila mtu hawezi kuweka wazi mshahara wake. Nanyi fanyeni mchakato wa kuingiziwa pesa zenu”

“Haya bwana”

Qeen akanifwata nilipo kaa na taratibu akanikalia mapajani mwangu huku akinitazama usoni kwa macho malegeu. Mapigo yangu ya moyo yakaanza kunienda kasi mara baada ya kumtazama kwa sekunde kadhaa kwani maneno ya Ethan aliyo niambia ni lazima niweze kumuua Qeen kwani anaweza kuwa adui yangu namba moja akiungana na maadui zangu, taratibu yakaanza kujirudia kichwani mwangu.



“Qeen tuweza kzungumza ”

Nilizungumza kwa sauti ya upole huku nikitazama usoni mwake.

“Sawa”

Tukaondoka hapa sebleni na kuingia kwenye moja ya chumba. Taratibu nikaegemea moja ya ukuta huku nikimtazama Qeen usoni mwake.

“Niambie Ethan mbona unanitazama tu halafu huzungumzi kitu cha aina yoyote?”

“Kwa nini unanipenda?”

Furaha ambayo imemtawala Qeen usoni mwake ikaanza kupungua. Akanyamaza kimya huku akinitazama kwa aibu.

“Ethan unajua….mi..mi……”

Qeen akabaki akiwa amejawa na kigugumizi kizito na kushindwa kuzungumza kama alivyo zungumza kipindi tukiwa ndani ya ndege.

“Natambua kwamba una nipenda ila naomba kitu kimoja kutoka kwako. Hakikisha unaweza kuzuia hisia zako kwangu. Sihitaji kukuumiza moyo wako wala nafsi zako. Nitazidi kukupenda kama mtu wangu wa karibu na si kimapenzi umenielewa?”

Qeen akanijibu kwa kutingisha kichwa huku machozi yakimwagika usoni mwake. Nikaanza kutembea kuelekea mlangoni ila Qeen akaniwahi kunishika mkono, akanivuta kwake na bila idhini yanguakaanza kuninyonya lipsi zangu.

“Qeen unafanya nini?”

Nilizungungumza huku nikijitahidi kujitoa mwilini mwake ila nikashindwa kufanya hivyo kwani amending’ang’ania kisawa sawa. Qeen akazidi kwenda mbali zaidi, akaanza kumpapasa jogoo wangu kwa kiganja cha mkono wake wa kulia. Tartibu jogoo wangu akaanza kujawa na hamu ya kuweza kuanzisha mashambulizi kwa Qeen.

Nikaivua suruali ya Qeen na kumuinamisha ukutani, jogoo wangu akaanza kutafuna kitumbua cha Qeen taratibu. Minung’uniko ya kimahaba nina uhakika wa asilimia mia moja inawafikia Latifa na Roman walio kaa sebleni. Baada ya dakika kadhaa tukamaliza mtanange huu, kila mtu akavaa nguo zake huku Qeen akiwa amejawa na furaha usoni mwake. Nikatoka chumbani hapa, sikuona hata haja ya kuendelea kukaa hapa, nikawaaga Latifa na Roman kasha nikaondoka. Moja kwa moja nikaelekea kwenye moja ya hoteli, nikakodisha chumba, nikaoga na kurudi nyumbani kwa mzee Poul Mkumbo. Nikawakuta wote sebleni huku nao wakiwa katika hali ya furaha.

“Ethan umesikia matokeo?”

Baba mkwe

“Ndio niliyasikiliza kupitia redio yangu ya ndani ya gari”

“Yaani nimefurahi sana huyu mwana haramu kukosa kiti cha uraisi. Angenisumbua sana pumbavu zake”

Mzee Poul Mkumbo alizungumza kwa furaha sana kiasi cha kunifanya nimcheke kimoyo moyo kwani kile kinacho kwenda kutokea yeye na mwezake kila mmoja atalia kwa namna yake.”

Habari katika televishion ya taifa zikabadilika na kutangaza juu ya kuanguka ukumbini na kupoteza fahamu

mgombea uraisi wa chama cha upinzani.

“Ohoo mshenzi alijiamini sana alihisi kwamba kujitoa kwangu yeye atashinda ehee?”

Mzee Poul Mkumbo alizungumza huku akiwa amejawa na furaha kubwa sana.

“Nahisi”

Nilizungumza nami huku nikimtazama baba mkwe.

“Sasa Ethan inabidi tutengeneze mfumo wa kujiweka karibu na huyu huyu mwana mama”

“Hilo ni wazo zuri baba”

“Yaa kwa maana nikijiweka karibu naye kuna mambo yangu mengi sana yatakwenda vizuri”

“Ila inabidi kama ni kumuingia tuweze kumuingia kwa siri sana, si unajua hivi sasa macho ya watu wengi

Yatakuwa yakimtazama kwa ukaribu sana?”

“Ni kweli inabidi ikiwezekana wewe ndio uanzishe mahusiano naye ya kuwa naye karibu”

Nikamtazama mzee Poul huku moyoni mwangu nikiwa nimestuka kidogo.

“Najua umenisaidia mengi sana mkwe wangu ila kwenye hili jambo ninakuomba usiweze kuniacha peke yangu.

Mimi na familia yangu bado tuna kutegemea kwa asilimia kubwa sana”

Mzee Poul Mkumbo alizungumza kwa kujitetea kwa maana kama ni mambo niliyo yafanya kwenye hii familia ni

mengi sana.

“Ila baba inabidi mume wangu sasa apumzike. Amekupigania kwenye mambo mengi sana bwana”

“Ni kweli baba Biyanka kumbuka huyu kijana wa watu moja si mwana sias, mbili ana majukumu ya kampuni zake

ambazo zote zina mtegemea yeye.”

Mama mkwe naye akanitetea, mzee mkumbo akanitazama kwa macho ya kukata tama juu ya ombi lake alilo

Niomba.

“Nitakusaidia baba”

“Ethan!!”

“Natambua mke wangu kila jambo linalo endelea. Kumbukeni kwamba tumetumia pesa nyingi sana kwenye haya

kampeni. Endapo hatuta jiweka karibu na huyu mama na kuhakikisha kwamba biashara zetu zina wigo mzuri

hakika tunakwenda kupoteza mambo mengi sana na inaweza kupelekea sisi kufilisika kiuchumi pia”

“Hili ndio nilikuwa nina lifikiria mkwe wangu. Hapo umefikiria kiume, tuna takiwa kurudisha garama zetu japo

nusu au munataka siku moja hapa tule miogo ya kuchemsha”

“Pia ni maisha”

Mama mkwe alizungumza kwa sauti ya upole na unyonge kidogo.

“Mmmm hiyo aibu nani anaitaka. Kutoka kuwa tajiri mkubwa hadi kuwa masikini nani anataka hayo mambo”

“Kwahiyo ikitokea hivyo mume wangu unahisi tutafanyaje?”

“Haiwezekani kutokea hivyo hata siku moja. Ethan mwanangu naomba uweze kunisaidia katika hilo”

“Sawa baba”

“Jamani sisi kesho tunarudi kwetu, kukaa hapa kwenu tumechoka”

Biyanka alizungumza huku akiwatazama wazazi wake.

“Kisha cha kuondoka ni nini?”

“Tumechoka tu, na sisi tunahitaji muda wa kupumzisha akili zetu, hatujui biashara zetu zinakwendaje”

“Sawa kikubwa muwe makini. Ethan ninaomba tuzungumze”

Tukaondoka sebleni hapa na baba mkwe, tukaingia ofisini kwake.

“Ndio mzee”

“Najua sasa muda wa mimi kuwa muwazi kwako umefika”

Nikastuka kidogo ila nikajitahidi kuhakikisha kwamba ninauzuia mstuko wangu kwake.

“Kivipi baba?”

“Kipindi cha ujana wangu nilipo hakikisha kwamba ninazidi kujiongezea uchumi wangu nilikuwa ninafanya kila

jambo kuhakikisha kuwa ninapata kile ninacho kikusudia”

Mzee Poul Mkumbo alizungumza kwa sauti ya upole sana huku akinitazama usoni mwangu.

“Sikuona shida kumuua mtu au watu ili niweze kuhakikisha kwamba ninapata kile ninacho kihitaji. Mikono yangu ina damu za watu wengi sana, mikono yangu imefanya mambo mengi sana mabaya na sihitaji ifikie siku uje kuyasikia mambo haya kutoka kwa watu wengine”

Maneno yam zee Mkumboyakanifanya nimkazie macho huku hasira ikianza kunipanda taratibu kwani yeye ndio mtu aliye husika kuondoa vifo vya wazazi wangu.

“Kwa nini unaniambia hayo yoyote baba”

Nilizungumza kwa msisitizo kidogo hukunikiendelea kukazia macho mzee Mkumbo.

“Wewe sasa ni sawa na mwanangu. Katika maisha yangu, Mungu amenijalia kupata binti mmoja, nilitamani kupata motto wa kiume ila hadi ninafikia umri huu sijaweza kupata mtoto wa kiume hivyo sina mtu ambaye ninaweza kumueleza mambo yangu ya ndani zaidi yako”

Nikajitahidi sana kuendelea kuizuia hasira yangu kwani tayari nimesha kunja ngumi yangu katika mkono wangu wa kulia na nina tamani sana kuhakikisha kwamba nina mshushia ngumi nzito kwenye uso wake.

“Nhaitaji unilinde sasa Ethan. Ninahitaji uweze kufahamu mali zangu zote na uendelee kuzilinda kama ninavyo jitahidi mimi kuzilinda.”

“Mali hizo ni halali?”

“Zipo nilizipata kihalali na nyingine nilizipata kifigisu figisu”

Nikashusha pumzi huku nikimtazama mzee Mkumbo kwa macho ya uchu wa kuhakikisha kwamba ninamuangusha mzee huyu kiuchumi hadi ajutie ni kwa nini amezaliwa katika dunia hii.

“Huoni hizo mali ulizo zipata katika njia ya short cut zinaweza kuniingiza mimi kwenye matatizo?”

“Hapana nilisha zitengenezea mazingira mazuri na hakuna mtu ambaye anafahamu kwamba si za halali kwa maana matukio niliyo yafanya ni ya miaka mingi sana ya nyuma.”

“Sawa, nitajitahidi kadri ya uwezo wangu kuziangalia mali zako”

“Nashukuru sana mwanangu. Tumepanga nama yako kwenda nje ya nchi kwa mapumziko, ila kabla ya kwenda nitajitahidi kuhakikisha kwamba ninakuonyesha mali zangu zote”

“Sawa mzee”

Nikatoka ofisini humu na moja kwa moja nikaelekea chumbani kwetu. Nikavua nguo zangu na kuingia bafuni, baada ya kuoga nikarudi ndani na kupanda kitandani.

“Hei mume wangu umelala bila hata ya kula?”

“Nimechoka sana mke wangu ninaomba niweze kupumzika”

“Jamani nina kuoenea huruma jinsi baba anavyo kubebesha majukumu mengi hadi yanakera”

“Usijali mke wangu”

“Muda mwengine ninakuonea huruma”

Biyanka alizungumza huku akikaa pembeni yangu.

“Vipi baba amekuambia nini?”

“Tutazungumza kesho nikiwa nipo sawa”

“Haya mume wangu”

***

Baada ya wiki moja mzee Poul Mkumbo akaanza kunitembeza katika makampuni yake anayo yamiliki huku kila kampuni akieleza ni jinsi gani alivyo ipata.

“Hii kampuni yangu haisafirishi samaki tu kwenda nje ya nchi”

Mzee Mkumbo alizungumza huku tukiwa kwenye godauni kubwa sana lililo jaa wafanyakazi wanao shuhulika na kuanda samaki walio toka kuvuliwa baharini.

“Kivipi mzee wangu sijakuelewa?”

“Njoo nikuonyeshe

Tukaingia katika moja ya mlango katika godauni hili huku mlangoni hapa kukiwa na walinzi wawili walio shika bunduki. Katika chumba hichi kikubwa tukakuta watu walio valia mavazi meupe tofauti na wafanyakazi walipo eneo tulilo tokea. Kitu kilicho nistusha sana ni pakti nyingi za madawa ya kulevya aina ya cocain ambazo zinaingizwa kwenye samaki wakubwa walipo humu ndani.

“Hii ni biashara ambayo inaniingizia kiasi kikubwa sana cha pesa”

“Unga!!?”

“Ndi mwanangu. Natambua kwamba wewe ni mfanya biashara na kila siku nina imani kwamba unakuwa unatamani kuongeza kiasi cha pesa kwenye himaya yako. Hivyo hata mimi huwa nipo vizuri katika hili, nina hakikisha kwamba ninajiongeza kiuchumi kadri ya siku zinavyo zidi kwenda”

Mzee Poul Mkumbo alizungumza kwa kujiamini sana jambo lililo nifanya nimshangae kwa maana laiti kama angepata uraisi sijui hii biashara angeitanua kwa kiasi gani.

“Sawa”

“Ila hii ni siri kubwa sana kwa wafanyakazi wangu hawa wachache.”

Nikaendelea kuwatazama wafanyakazi hawa wanacho kifanya ubaya ni kwamba wamezificha sura zao na ningumu sana kwa kuweza kumshika hata mmoja wao kisura.

“Hii biashara inakuingizia kiasi gani cha pesa baba?”

“Kwa mwaka inaniiingizia zaidi ya dola za kimarekani bilioni tano hadi saba”

“Duuu kwa hiyo ina pesa nyingi ehee?”

“Ndio maana nikakuonyesha. Hizi biashara nyingine kwangu ni kama kivuli ila hii ndio kila kitu. Uzuri kwamba mimi ndio ninatangeneza cocain hamu ndani kuna wa professional kutoka Colombia ambao nimewapa kazi hiyo ya kuzalisha cocain grade one ambayo ndio ina pesa na inatumiwa na watu matajiri tu.”

“Kumbe cocain ina grade?”

“Ndio kuna grade one, grade two, grade three hiyo ndio inatumiwa na watu wengi wa bara hili la afrika”

“Sawa”

Mzee Poul Mkumbo akanitambulisha kwa baadhi ya wasimamizi wake wa biashara hii haramu.

“Akihitaji kufanya biashara hii mkwe wewe nijulishe nitakuingiza uweze kuifanya kiumakini n itazidi kukuongezea kipato kikubwa”

Mzee Poul Mkumbo alizungumza huku tukingia kwenye gari tulilo jia. Sikumjibu kitu chochote huku akilini mwangu nikianza kupanga ni jinsi gani nitazidi kumfelisha mzee huyu na kitu cha muhimu ambacho kwa sasa nina hitaji niweze kukipata ni vitabu vyake vyote vya benki ambavyo vinaweza kuniwezesha kuzijua akauti zake na nitajua ni jinsi gani nitakavyo weza kuzifunga na kuziiba pesa zote.

“Alafu kuna jambo bado baba hujanipatia ripoti”

“Jambo gani?”

“Yule mpinzani wako vipi umeweza kumchukulia hatua juu ya matukio yake ambayo ameyafanya kwako?”

“Bado ila najua ni wapi nitambana na ninasikia fununu fununu kwamba wanahitaji kupinga matokea ya uraisi hivyo nitahakikisha kwamba ninambana kuhakikisha kwamba hakurupuki katika jambo hilo”

“Basi kama ni hivvyo sawa”

“Yaa tukiondoka mimi na mama yanu kwenda mapumzikononi, tukirudi nahiji muweze kufunga ndoa sawa”

“Sawa”

Nilijibu kwa unyonge huku nikimtazama mzee Poul Mkumbo usoni mwake kwani sina mpango wa kumuoa mwanangu. Tukafika katika eneo kubwa la mgodi wa mzee Poul Mkumbo, nikaanza kulitazama eneo hili na machozi yakaanza kunilenga lenga kwa maana ndio eneo lilipo kuwa shamba letu kubwa la migomba.

“Ukiachana na ile biashara yangu niliyo kuonyesha ya kwanza. Hii ndio biashara yangu nyingine inayo niingizia pesa nyingi sana.”

“Uliiupataje huu mgodi?”

Nilimuuliza mzee Poul Mkumbo kwa msisitizo hadi yeye mwenyewe akanitazama kwa mshangao kwani si kawaida kwa mimi kumuuliza kwa mtindo huu.



Mzee Poul Mkumbo akashusha pumzi taratibu huku akiendelea kunitazama usoni mwangu.

“Nitakueleza kijana wangu”

Mzee Poul Mkumbo alizungumza kwa kujiamini, tukapokelewa mzee mmoja wa kizungu na tukakabidhiwa kofia ngumu maalumu kwa ajili ya kujikinga na ajali zote zinazo weza kutupata katika vichwa vyetu. Pia tukakabidhiwa na makoti maalumu yenye rangi ya kijani yanayo ng’ara sana mtu akiwa gizani. Tukaanza kutembea maeneo mbalimbali ndani ya eneo hili la mgodi huku nikiendelea kuonyeshwa jinsi madini yanavyo chimbwa na mitambo mikubwa iliyo fungwa katika mgodi huu. Matembezi haya yakatuchukua kama lisaa moja na nusu hivi kisha tukatoka ndani humu huku hamu kubwa ya kuuchukua mdogo huu ikiendelea kunijaa moyoni mwangu. Tukaondoka katika mgodi huu pasipo kuzungumzia jambo lolote. Tukafika kwenye moja ya hoteli kubwa yenye hadhi ya nyota tano.

“Leo ninataka kukutambulisha kwa wachimbaji wakubwa wa migodi hapa Tanzania na Afrika nzima”

Mzee Poul Mkumbo alizungumza huku akinitazama usoni mwangu. Tukaingia kwenye moja ya ukumbi na kukuta watu walio valia suti nyeusi huku wengi wao kwa mtazamo wa haraka haraka wanaonekana ni watu wenye pesa nyingi sana na wengi wao nina hisi pesa zao utafutaji wake wanafanya kama mzee Poul Mkumbo. Wakanyanyuka na kumsalimia mzee Poul Mkumbo kwa heshima sana.

“Huyu ni kijana ni mkwe wangu. Pia ni mfanya biashara nina imani kwamba baadhi yenu mutakuwa muna mfahamu”

Nikaona baadhi yao wakitingisha vichwa wakimaanisha kwa mba wana nifahamu. Baada ya utambulisho huo mzee Poul Mkumbo akaniomba niweze kutoka nje ili waweze kufanya kikao na wafanya biashara hawa. Dada mmoja amabye ni muhudumu wa hii hoteli akanichukua hadi kwenye chumba cha kupumzikia.

“Utatumia kinywaji gani?”

“Ninahitaji maji tu”

“Yabaridi au ya moto?”

“Maji ya moto”

“Sawa”

Muhudumu huyu akatoka na kuniacha peke yangu humu chumbani. Baada ya muda akarudi akiwa na chupa kubwa ya maji, akataka kuifungua ila nikamzuia na kumuomba aiweke juu ya meza ya kioo iliyo humu chumbani.

“Kitu kingine unahitaji muheshimiwa?”

“Hapana sihitaji chochote”

“Sawa”

Msichana huyu akafungua mlango na kutoka chumbani hapa. Gafla nikamuona Ethan akiwa amesimama pembeni ya meza, akachukua maji haya na kuyasoma.

“Unaonekana huna gadhabu kubwa sana juu ya baba yako mkwe?”

Nikashusha pumzi taratibu huku nikimtazama Ethan usoni mwake.

“Yaa”

“Nimekuja kukuchukua ukaone jambo fulani”

“Jambo gani”

“Wewe twende”

Ethan akanishika mkono na gafla tukatokea kwenye eneo la mgodi ila sehemu yenye moja yam lima mkubwa ambao unatufanya tuweze kuuona mgodi huu kwa chini.

“Huu mlima una ukumbuka?”

Ethan aliniuliza huku tukiendelea kutazama eneo la mgodi. Nikaendelea kuutazama mlima huu na nikatingisha kichwa nikimaanisha kwamba nina ukumbuka huu mlima. Ethan akakipitisha kiganja chake cha mkono wa kulia katika uso wangu. Kufumba na kufumbua giza kubwa likatawala katika eneo hili. Mvua iliyo ambatana na radi ikaendelea kutawala. Sikuweza kuona mgodi huu zaidi ya migomba mingi.

“Unawaona wale”

Ethan alizungumza huku akiwanyooshea vidole vijana fulani walio izunguka nyumba ndogo. Vijana hawa nikawakumbuka kwa haraka na hawa ndio vijana ambao walimshambulia baba yangu na wao ndio walitukimbiza mimi na mama yangu na kututenganisha kuanzia hapo na sikuweza kuishi na wazazi wangu walio nizaa.

“Kwa nini una nionyesha vijana hawa”

“Twende”

Tukashuka kwenye mlima huuna kusimama pembeni ya vijana hawa ambao nina shuhudia jinsi wanavyo mshambulia kwa kumpiga baba yangu. Hasira na chuki vikazidi kunijaa juu ya mzee Poul Mkumbo kwani yeye ndio mtu wa aliye mpiga baba yangu risasi kadhaa kifuani mwake huku vijana alio waagiza kutufukuzia wakurudi wakiwa na mama yangu anaye lia kwa uchungu sana.

“Ehee yule mtoto mume mpata?”

“Ndio tumemtupia kwenye maporomoko ya mlima na tuna imani kwamba atakuwa amekufa kabisa.”

“Kazi nzuri na huyo mwana mama?”

“Ni mke wa huyu mzee”

Mzee Mkumbo akamtazama mama yangu kisha akapiga na yeye risasi kadhaa za kifuani na mama yangu akapoteza maisha hapa hapa.

“Huu ndio ukweli wa kifo cha wazazi wako. Sikuhitaji kukuonyesha kipindi ukiwa mtoto kwa maana haukuwa na nguvu kabisa ya kuweza kupambana na adui yako”

Ethan alizungumza na kunifanya machozi yazidi kunimwagika usoni mwangu.

“Nahitaji kumuua mzee Poul Mkumbo kama jinsi alivyo waau wazazi wangu”

“Unatakiwa kuwa mvumilivu ila hii ni vita vita anbayo sasa ndio umeingia rasmi. Ile mipango uliyo kuwa una ifanya kumuondoka kwenye nafasi ya uraisi zile zilikuwa ni rasha rasha.”

“Unaziona hizi sura?”

Ethan alinionyesha sura za vijana wote walio husika katika mauaji ya wazazi wangu. Nikawatazama watu hawa na sura zao kwa haraka zikanikaa kichwani mwangu.

“Umewaona?”

“Ndio nimewaona”

“Sasa hawa ndio unatakiwa uanze nao”

“Wapo nchini hapa Tanzania?”

“Ndio na kila mmoja nitakuonyesha na wewe ndio unatakiwa uweze kuifanya hii kazi usikabizi mtu wa aina yoyote kwa maana hii kazi ni kazi inahusiana na damu ya wazazi wako”

“Nashukuru kusikia hivyo”

“Ila hakikisha kwamba kila kichwa cha mtu ambaye una muua mzee Poul Mkumbo kina mfikia”

“Kitamfikia vipi Ethan”

“Usijali utajua ni jinsi gani unavyo weza kumpata”

Ethan akapitisha tena kiganja chake usoni mwangu na kufumba na kufumbua nikajikuta nikiwa katika chumba cha hoteli ambacho nilikuwepo. Hata kabla ya dakika moja kuisha akainagia mzee Poul Mkumbo huku akiwa na furaha sana moyoni mwake.

“Ehee kijana wangu pole sana kwa kukaa mwenyewe kwa dakika kadhaa hizi”

“Usijali baba”

“Sasa leo tutalala kwenye hii hoteli na kesho tutarudi jijini Dar es Salaam au unasemaje?”

“Hakuna shida”

“Basi twende ukaone chumba chako kisha mida ya jioni hivi kuna viongozi fulani hivi tunaweza kupata nao chakula cha usiku. Nahitaji nizidi kukuunganisha kwa hawa viongozi kwa maana nina imani kwa kupitia wao biashara zetu zote ulizo weza kuzishuhudia kwa siki ya leo zitekwenda vizuri sana.

“Nimekuelewa baba mkwe”

Tukatoka chumbani humu na kupandisha gorofa ya saba ambayo ndio gorofa ya mwisho kabisa ya hoteli hii. Kila mmojaa akakabidhiwa chumba chake, nikaingia chumbani kwangu na nikakigua na nilipo weza kufanikiwa kukikagua na kufahamu kwamba kipo salama. Nikaingia bafuni, ila kabla ya kuoga nikamuona Ethan akiwa amesimama nyuma yangu huku akiwa ameshika nguo mkononi mwake.

“Zijaribishe nguo hizi?”

Nikageuka na kuzitama nguo hizi, nikazichukua na kuvua nguo nilizo zivaa, nikazijaribisha. Nguo hizi zimeshinishika vizuri mwili wangu na zinavutika vizuri sana.

“Hizi nguo ni nzuri kwa kazi unayo kwenda kuifanya na hizi ni gloves ambazo unaweza kuzivaa katika kazi yako unayo kwenda kuifanya”

“Ni nzuri nimezipenda”

“Usiku nitakuletea silaha maamuli ambayo utatakiwa kuifanya. Ila hakikisha kwamba hakuna mtu ambaye anaweza kuziona hizo nguo zako”

“Nimekuelewa”

Ethan akaondoka ndani hapa, simu yangu ikaanza kuita nikaitoa na kukuta ni namba ya Biyanka, nikaitazama kwa sekunde kadha kisha nikaipokea.

“Mume wangu mbona leo umenisusa sana au ndio huko kutembezwa na baba?”

“Yaa tumetembea sana na baba leo ndio maana umeona nipo kimya”

“Vipi lakini umeweza kufahamu maeneo yote?”

“Yaa kiasi nimeweza kufahamu”

“Sawa mume wangu ila hakikisha kwamba unakuwa salama sawa”

“Poa mke wangu”

“Basi baadae”

“Sawa mke wangu”

Nikakata simu na kuanza kufikiria ni jinsi gani ninavyo weza kuifanya hii kazi. Usikuw asiku ya leo nikakutana na viongozi baadhi wa serikalini na tukapata chakula cha usiku kisha nikamuomba mzee Poul Mkumbo niweze kupumzika mapema kwa maana sijisikii vizuri. Mzee Pouk kumbo akaniita pembeni na tukasimama kwa pamoja.

“Leo usiku kuna vitoto vibichi vibichi nitalala navyo ila ninaomba usimueleze mama yako juu ya hivi vibinti”

Mzee Poul Mkumbo alizungumza huku akinionyesha wadada wawili. Nikatabasamu huku nikimtazama usoni mwangu.

“Wala usijali mzee wangu mimi ni mwanaume nina elewa”

“Sawa kampumzike kijana wangu.”

Nikaachana nao na kuelekea chumbani kwangu. Nikamkuta Ethan akiwa amesimama pembeni ya kitanda changu huku akiwa ameshika upanga mmoja unao ngara vizuri na wenye uwefu kiasi na wembaba.

“Hakikisha kwamba hili swador unaitumia vizuri. Umenielewa?”

Ethan alizungumza huku akinikabidhi upanga huu, taratibu nikajikuta nikianza kujawa na roho ya chuki, roho yenye hamu ya kulipiza kisasi na roho ambayo hakika nitahakikisha kwamba kila adui yangu ambaye nitampata nitahakikisha ninamsambaratisha kama jinsi wao walivyo nisambaratisha na wazazi wangu.



“Ndio nimekuelewa”

“Safi, sasa tunakwenda pamoja. Umenielewa?”

“Yaaa”

Ethan akanishika mkono na fumba na kufumbua tukajikuta tukiwa kwenye barabara ya lami iliyo tulia huku nyumba zilizopo karibu na barabara hii zikiwa zimejengewa kuta kubwa pamoja na mageti makubwa mazuri na dhairi inaonyesha kwmaba eneo hili watu wanao ishi ni matajiri na wenye fedha nyingi sana.

“Kwa nini tupo hapa?”

Nilimuuliza Ethan huku nikimtazama usoni mwake.

“Subiri kidogo”

Ethan alizungumza huku tukiwa tumesimama katikati ya barabara. Baada ya dakika kama mbili tukaona gari la ndogo aina ya Toyota Brevis, ikija kwa kasi sana katika barabara hii. Jinsi gari hili linavyo zidi kuja kwa kasi likanifanya nijawe na wasiwasi mkubwa sana kwani dereva huyu anaweza kutugonga. Nikataka kuondoka barabarani ila Ethan akanishika mkono. Dereva wa gari hili gafla akatukwepa, ila kutukwepa kwake akashindwa kulihimili gari lake na kujikuta akiingia mtaroni mzima mzima.

“Kwa nini tumemsababishia ajali mtu ambaye hatuna nia naye”

Ethan hakunijibu kitu chochote zaidi ya kuniachia mkono wangu. Akaanza kutembea hadi lilipo gari hili, akafungua mlango wa upande wa dereva na kumtoa mwanaume ambaye kwa haraka nilivyo mtazama nikamgundua. Ni mmoja wa vijana aliiye pendekeza wazo la kumbaka mama yangu.

“Mchinje”

Ethan alizungumza huku akinitazama usoni mwangu. Jamaa huyu japo amepata ajali mbaya ila yupo hai na macho yake yaanitazama vizuri.

“Unasubiri nini Ettha fanya kazi iliy tuleta hapa”

Ethan aliendelea kusisitiza niweze kufanya ukatilia ambao nilijiapiza ni lazima niweze kuufanya kwa wale wote walio husika katika kumua baba yangu na mama yangu. Nikauchomoa upanga huu mrefu taratibu kwenye sehemu yake ulipo chomekwa. Nikamtazama jamaa huyu na bila ya huruma nikaushusha upanga huu shingoni mwake na kukitengenisha kichwa na kiwili wili chake.

“Safi”

Ethan alizungumza huku akiookota kichwa cha jamaa huyu. Etthan akafungua buti ya gari hili na kutoa mfuko wa nailoni na kukiingiza kichwa cha maja huyu.

“Cha nini hicho kichwa?”

“Tunaondoka nacho”

“Kwa nini?”

“Mara moja hii umesahau niliyo kuwa nimekuambia.?”

Swali la Ethan likanikumbusha maneno yake ya kubwa, nilazima mzee Poul Mkumbo aweze kuhushuhudia vichwa vya watu wake wote walio husika katika kusimbaratisha familia yangu. Ethan akanishika mkono na kuondoka eneo hili, tukatokea katika eneo jengine ambalo limetulia sana na nyumba zake zimejitenga sana kutoka kwa jirani mmoja hadi mwengine.

“Tunaingia katika nyumba hiyo”

Ethan alizungumza huku akinionyesha nyumba ya kawaida tu iliyopo mbele yetu.

“Ndio”

Ethan akaendelea kunishika mkono wangu. Kwa uwezo wake alio nao tukajukuta tukiwa ndani ya chumba kimoja chenye kitanda cha wastani huku kukiwa na mwanaume mwengine ambaye naye niliweza kumfahamu kwnai naye ni mshiriki wa tukio lililo tokea miaka mingi sana ya nyuma juu ya familia yangu japo ni miaka mingi imepita ila nina wakumbuka vizuri sana.

“Mchinje”

“Hapa kitandani kwake?”

“Ndio unaogopa nini?”

Nikajifikiria kwa muda, nikaushika upanga huu vizuri kisha nikaushusha kwa nguvu shingoni mwake na kusababisha damu nyinngi sana kuturukia mwilini mwetu huku kiwili wili chake kikianza kucheza cheza mithili ya kuku aliye chinjwa kisha akaachiwa apapaparike.

“Safi”

Ethan alizungmza huku akichukua chumba cha mtu huyu na kukiingiza kwenye mfuko.

“Kwa hapa Moshi tumesha tuondoke”

Ethan akanishika mkono na hata dakika moja haikuweza kuisha tukajikuta tukiwa ndani ya chumba changu cha hoteli.

“Ninakwenda kuviweka hivi vichwa ndani ya chumba cha mkweo”

“Sasa hivi?”

“Ndio, akiamka asubuhi ataviona”

“Sawa”

Ethan kwa ishara akaniomba nimkabidhi upanga huu pamoja na nguo hizi za kazi alizo vivaa. Nikafanya hivyo kisha akatoweka chumbani humu. Nikaingia bafuni nikaoga huku nikiusafisha mwili wangu vizuri sana na nilipo maliza nikapanda kitandani na kila ninavyo jaribu kuutafuta usingizi nikajikuta nikishindwa kabisa. Nikachukua simu yangu, nikampigia Camila kwa kupitia mtandoa wa Imo. Baada ya sekunde kadhaa simu yake kuita, Camila aiakipokea na tukaanza kuzungumza huku tukionana.

“Niambie mume wangu”

“Safi vipi umevalia suti unakwenda wapi?”

“Huwezi amini mume wangu sasa hivi nimepata kazi katika kampuni ya BMW. Nimekuwa ni miongoni mwa mameja”

“Mmmm hongera”

“Mbona sasa unaguna baba watoto?”

“Hukuwahi kunieleza jambo kama hilo kwamba umeomba kazi na umepata kazi na kama ingekuwa si kukupigia nina hisi kwamba ungeanza kazi bila hata ya mimi kuweza kufahamu.”

“Samahani mume wangu kwa hili nimefanya kazi ila sababu ya kuweza kufanya hivi sikuhitaji kukusumbua kwenye harakati zako ambazo unaendelea kuzifanya huko nchini Tanzania.”

Camila alizungumza kwa suati ya upole huku akinitazama usoni mwangu.

“Haya sawa ila muda mwengine sinto penda mambo kama haya yaweze kujitokeza. Kumbu wewe ni mke wangu na nina kampuni nyingi sana ambazo unaweza kusimama kama msimamizi mkubwa”

“Nalitambu hilo mume wangu ila kumbuka nilisha wahi kukuambia sinto penda kufanya kazi katika kampuni za watu ambao ninawafahamu ikiwemo wewe mume wangu. Ndio maana watu wengi wananishangaa mimi kufanya kazi kwenye kampuni hii ikiwa wewe mume wangu ni mmiliki wa makampuni mengi huku baba yangu akiwa ni raisi wa hii nchi”

“Sawa nimekuelewa. Wanakulipa kiasi gani kwa mwenzi?”

“Dola laki mbili na nusu”

“Kwa muda gani?”

“Wiki”

“So ni one milioni dolar kwa mwenzi?”

“Ndio mume wangu”

“Sio mbaya ila msharaha bado haupo sawa”

“Mmm mume wangu una nitosha sana. Kumbuka maisha yangu sijalelewa kwenye shida wala matatizo ya aina yoyote hata hivyo asilimia ishirini na tano nimeitoa kwa ajili ya watoto wote wanai ishi maisha ya shida barani Asia”

“Ni jambo zuri pia hilo mke wangu.”

“Nashukuru mume wangu. Ila mbona kama unaonekana huna furaha. Una umwa?”

“Hapana”

“Una nini mume wangu?”

“Sina kitu”

“Hapana Ethan una nidangaya. Ninakufahamu vizuri sana, hembu nitazame usoni mwangu”

Nikamtazama Camila ila kusema kweli akili yangu haipo sawa, kwani swala la kumuua binadamu mwenzangu ni zito sana japo si mara yangu ya kwanza kufanya hivi ila hili swala lina uzito wake kwani kumchinja mtu kama ndege ni tofauti sana na kumpiga kwa kutumia risasi.

“Una tatizo Ethan niambie.”

Camila alizungumza kwa sauti ya upole na iliyo jaa mahaba mazito ya kunibembeleza.

“Camila”

“Beee”

“Una nipenda?”

“Ndio ninakupenda mume wangu ndio maana nipo nawe na nina kujali kwa kila jambo liwe zuri au baya mimi nipo pamoja nawe”

Nikashusha pumzi yangu taratibu huku nikimtazama Camila usoni mwake.

“Mazungumzo yetu yapo salama?”

“Ndio yapo salama mume wangu hakuna mtu anaye weza ku hack mazungumzo yetu”

Nikamtazama Camila jinsi alivyo jawa na shauku ya kuhitaji kufahamu ni kitu gani kinacho nisumbua.

“Nimeua watu mpenzi wangu”

Camila akastuka kidogo huku akinitazama kwa mshangao mkubwa sana.

“Kivipi na kwa nini?”

“Ni watu walio niulia wazazi wangu, baba na mama na wao ndio walishiriki katika kumbaka mama yangu”

Camila akaka kimya huku machozi yakimlenga lenga usoni mwake. Nikashindwa kujivumilia na kujikuta nikianza kulia kwa uchungu sana kwa vifo vya wazazi wangu hakika vimenifanya maisha yangu yote kuishi na roho ya kuhitaji kulipiza kisasi.

“Ethan natambua jambo ulilo lifanya sio kosa. Umewapa haki walio stahili kuweza kuipata kutoka kwako kwa maana haiwezekani waweze kufanya matukio hayo nawe uweze kuwaacha hai wakiendelea kula maisha katika hii dunia. Kwahilo mume wangu nina kuunga mkono na kama bado wapo wengine walio salia, kill them all”

Camila alizungumza kwa ukakamavu na kwa ujasiri mkubwa sana huku akinitazama usoni mwangu. Maneno ya Camila yakaamsha hisia zangu za ujasiri, swala la kujilaumu kwa kufanya mauaji haya likapotea kabisa.

“Unaweza kuitunza siri hii mke wangu?”

“Asilimia mia moja mume wangu. Ni mambo mangapi tumefanya mume wangu. Ulisha wahi kuyasikia hata yakizungumzwa na watu?”

“Hapana sijasikia”

“Basi amini kwamba siri yako kwangu ipo salama mume wangu”

“Nashukuru nitahakikisha hii kazi nina imaliza na ikiisha nitahakikisha kwamba tunafunga ndoa na ninarudi uwanjani kuifanya kazi ninayo ipenda toka nilipo kuwa mtoto mdogo.”

“Sawa mume wangu. Ninakuahidi kukuunga mkono kwa kila jambo na niahitahi hata leo tuweze kufunga ndoa ila hali ya mambo ndio inatuweka mbali kwa sasa”

“Nashukuru kwa kunifariji mke wangu, ngoja nilale kwa maana huku ni usiku sana”

“Sawa mume wangu acha mimi nijiandae niwahi kazini nisije nikachelewa kwa maana leo hii ndio kwanza ni siku ya kwanza”

“Poa nakupenda sana Camila”

“Nakupenda pia Ethan wangu”

“Nashukuru”

Mazungumzo yetu yakaishia hapa, nikakata simu na kuiweka pembeni. Taratibu nikavuta shuka hili zito na kujifunika na taratibu usingizi ukaanza kunipitia na nikalala fofofo.

***

Sauti ya mlango unao gongwa kwa nguvu ikanistua sana usingizini, nikautazama mlango huu wa chumba changu na mtu huyo akendelea kugonga kwa nguvu. Wasiwasi ulio changanyikana na woga vikanitawala, nikashuka kitandani mwangu na kunuyata hadi mlangoni. Uzuri wa mlango huu una kitobo ambacho kinamuwezesha mtu wa ndani kumuna vizuri mtu wa nje ila mtu wa nje hawezi kumuona mtu wa ndani. Sikuamini macho yangu mara baada ya kumuona mzee Poul Mkumbo akiwa amesimama mlangoni huku akiwa uchi kama alivyo zaliwa, kwa haraka nikaufungua mlango huu na mzee Poul Mkumbo akaingia ndani humu kwa kasi kana kwamba anakimbizwa.

“Baba kuna nini tatizo”

“Ethan kuna vichwa ndani kwangu”

Mzee Mkumbo alizungumza hukua akitetemeka sana. Kimoyo moyo nikaanza kucheka japo sijui ni jinsi gani Ethan alivyo weza kuviweka vichwa hivyo hadi kufikia hatua ya mzee Poul Mkumbo kuchanganyikiwa kwa kiasi hichi.

“Hembu tulia baba. Umesema kuna nini?”

Nilijifanya kumuuliza Poul Mkumbo kana kwamba sifahamu kitu kinacho endelea. Nikachukua taulo na kulabidhi mzee Poul Mkumbo ili aweze kujistiri zake za siri kwani hata kama ni mwanaume mwenzangu ila si vizuri kuona sehemu zake za siri na isitoshe ni baba yangu mkwe.

“Kuna vichwa vya watu walio chinjwa vimewekwa kitandani kwangu na wale wasichana wawili nilio lala nao siwaoni kabisa zaidi ya hivyo vichwa.”

“Mmmm acha kunitania baba?”

“Haki ya Mungu, Ethan sina utani na wewe mke wangu. Ila kweli wewe nenda ukajionee”

Nikachukua suruali yangu na tisheti nikavaa kisha nikatoka ndani kwangu. Nikaingia katika chumba cha mzee Poul Mkumbo, sikuamini kuona vichwa hivyo vikiwa kitandani mwake huku shuka jeupe la kitanda hichi likiwa limejawa na damu nyingi sana.

“Unaona unaona Ethan”

Mzee Poul Mkumbo alizungumza huku akinyoosha kidole kitandani mwake.

“Mzee unahisi vimetoka wapi hivi vichwa”

“Utalipa POUL MKUMBOOOOOO HAHAHAAAA………….!!!!”

Sote tulishutka mara baada ya kusikia suati ya baba yangu ikitokea kwenye vichwa hivyo vilivyopo kitandani huku vyote vikianza kucheka japo havina viwili wili jambo lililo mpelekea baba mkwe kuanguka chini mzima mzima huku haja ndogo ikimtoka na kulowanisha taulo nililo mkabidhi kujistiri.



Nikatamani kutoka ndani ya chumba hichi ila nikajikaza na kusubiria niweze kuona ni jambo gani ambalo linaweza kutokea juu ya hivi vichwa. Muhudumu aliye katiza kwenye kordo hii mara baada ya kumuona mzee Poul Mkumbo amenaguka chini kwa haraka akaingia ndini humu naye alipo kuta vichwa hivi vinavyo endelea kucheka kitandani, akatoka nje ya chumba hichi kwa haraka pasipo hata kutuaga.

“Ethan ni nini hiii jamani”

Mzee Poul Mkumbo alizungumza huku akiendelea kujawa na wasiwasi pamoja na woga mkubwa sana. Wakaingia wahudumu wengine watatu pamoja na askari wa hii hoteli wawili. Kila mmoja akazidi kujawa na mshangao kwa kuona vichwa hivi vikiendelea kucheka.

“UTAKWISHAAAAAA”

Mara baada ya vichwa hivi kuzungumza hivi vikanyamaza. Watu wote tukatazamana kwenye nyuso zetu huku kila mmoja akisubirini ni nani wa kwenda kuanza kuvitazama vichwa hivyo.

“Ehee hapo ni kituo cha polisi cha kati?”

Jamaa mmoja alizungumza huku akihangaika hangaika ndani ya chumba hichi.

“Munazungumza Edwin ni meneja wa hoteli ya Simanjiro. Kuna tukio la mauaji limetoka katika hoteli yangu hapa ninaomba msaada wenu”

“Haya sawa”

Kijana huyu akakata simu na sote tukabaki tukimtazama.

“Mzee”

Watu wote sasa ndio tukajikuta tukimfwatilia mzee Poul Mkumbo ambaye bado amelala chini. Tukasaidiana na watu hawa kumnyanyua na kumkalisha kwenye moja ya kiti kilichomo humu ndani.

“Mleteeni mzee maji ya baridi”

Meneja wa hii hoteli alizungumza huku sote tukimtazama mzee Poul Mkumbo aliye pooza mithili ya mtu ambaye amenusurika kupata ajali iliyo mpunyua punyua kutoa uhai wake. Tukiwa katika hali ya kumsaidia mzee Poul Mkumbo arudi katika hali ya kawaida, nikamuona Ethan akiwa amesimama pembeni ya kitanda hichi, nikawatazama watu wengine ila wote hakuna anaye onyesha kujua juu ya uwepo wa Ethan ndani ya chumba hichi. Ethan akatabasamu kisha akachukua vichwa hivyo na kubadilisha shuka la kitanda hicho na kuondoka eneo hili. Watu baadhi wakaanza kustuka baada ya kuona kitanda kikiwa kimetandikwa vizuri na vichwa hivyo vikiwa havipo kabisa katika neo hili.

“Ni macho yangu au?”

Kijana mwengine alizungumza huku akiwa amejawa na mshangao mkubwa sana. Watu wote wakaendelea kujiuliza maswali ambayo asilimia tisina na tisa ya maswali hayo mimi ndio mwenye majibu halisi. Askari wakafika chumbani hapa na hata walipo elezwa juu ya jambo lililo tokea wakabaki wakiwa wamejawa na mshangao huku wengine wakishindwa kuamini kabisa. Wakamuomba mzee Poul Mkumbo akaoge ili apatiwe ulinzi wa kuondoka hapa na kurudi jijini Dar es Salaam. Nikarudi chumbani kwangu huku nikiwa na furaha kubwa kiasi kwani hii vita ya kumuathiri mzee Poul Mkumbo kisaikolojia. Nikiwa bafuni, Ethan akatokea nyuma yangu.

“Naona jambo dogo tu mzee wako amejawa na jamba jamba kishenzi”

Ethan alizungumza huku akicheka sana.

“Hii plan pale awali sikuweza kuifikiria. Ninaona inafanya kazi ila kumtesa huku si kuzuri”

“Sio kuzuri kivipi?”

“Lengo langu katika maisha yangu ilikuwa ni kutafuta nguvu. Nimeipata nguvu ya pesa, sasa hivi ninacho hitaji kukifanya ni kuhakikisha kwamba mzee Poul Mkumbo anashuka kiuchumi na kula miogo kama wananchi wa hali ya chini kabisa. Huo ndio ulikuwa mpango wangu kwake”

Ethan akatingisha kichwa huku akionekana kukubaliana na kile ambacho nina kizungumza.

“Ila tukisha muharibu kisaikolojia ni muda wa kwenda kumfilisi kirahisi”

“Sawa ni wazo zuri”

“Pao mpango wetu utaendelea kila mara ambapo tutapata muda wa kuutekeleza ila si wazo zuri kumueleza Camila kila jambo katika huu mpamgo”

“Kwa nini ikiwa yeye ni mke wangu?”

“Natambua kwamba ni mke wako na unampenda sana, ila tambua kwamba endapo siku mukija kupishana kihisi anaweza kuyamwaga mambo yako mengi hadharani”

“Poa nimekuelewa”

Ethan akatoweka bafuni humu. Baada ya kumaliza kujiandaa nikaelekea chumbanik wa mzee Poul Mkumbo na kumkuta na R.P.C wa mkoa huu wa mkoa huu wa Moshi. Nikasalimiana na mzee huyu.

“Vipi baba?”

Nilimuuliza mzee Poul Mkumbo anaye vaa shati lake kwa unyonge mkubwa sana.

“Ehee?”

“Mzee bado hayupo sawa, tunahitaji kumpelekea hapo KCMC ili kupima presha yake ili tuweze kufahamu kama yupo sawa au laa”

R.p.c alizungumza kwa upole huku akinitazama kwa upole.

“Sawa, ila inabidi niwasiliane na mama”

Mzee Poul Mkumbo akaninyooshea mkono wake wa kulia ikiwa ni ishara ya kunikataza nisifanye jambo hilo. Mzee Mkumbo alipo maliza kujiandaa tukatoka nje na kuingia kwenye gari letu huku ulinzi wa askari ukiwa umeimarika sana. Tukafika katika hospitali hii na mzee Poul Mkumbo akapelekwa moja kwa moja kwenye chumba cha matibabu.

“Ilikuwaje kijana?”

Mkuu wa polisi mkoa huu wa Moshi aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.

“Mmmm…ni jambo la kushangaza kwa kweli”

“Unataka kuniambia na wewe uliweza kuviona hivyo vichwa?”

“Ndio, si mimi tu hata wale wafanyakazi wa pale hotelini waliweza kuviona na ni vichwa vya watu kabisa na vilikuwa vikicheka”

“Mmmm unataka kuniambia kwamba hili swala tuhusishe maswala ya mazingara?”

“Sijui ni swala gani, ila kusema kweli ni jambo linalo tish……”

Kabla sijazungumza kitu chochote, simu yangu ikaita, nikaitoa mfukoni, nikaona jina la madam Raisi Tasiana. Kwaishara nikamuomba mkuu huyu wa polisi nizungumze pembeni kidogo. Nikasogea hatua kadha ambazo si rahisi kwa mkuu huyu wa polisi kuweza kuzungumza chochote.

“Mama”

“Ndio mwanangu hujambo wewe?”

“Nipo salama mama yangu.”

“Nimesikia upo hapa Moshi ila hata kuja kunitembelea kwangu jamani?”

Nikashusha pumzi taratibu huku nikitafakari ni jambo gani ninaweza kumueleza mwana mama huyu.

“Ni kweli mama”

“Na KCMC unafanya nini?”

“Ahaa…nipo na mzee kidogo hali yake sio nzuri ndio maana nipo hapa”

“Sawa, unaweza kuja nyumbani kwangu?”

“Leo?”

“Muda huu?”

Nikamtazama R.P.C anaye zungumza na vijana wake walio imarisha ulinzi nje ya chumba anacho fanyiwa matibau mzee Poul Mkumbo.

“Ahaaa mzee yupo kwenye chumba cha matibabu ila unaweza nipa dakika kadhaa nikajua ripoti kutoka kwa madaktari kisha nitakuja kwako”

“Sawa fanya hivyo kijana wangu”

Nikakata simu na kurudi eneo la chumba.

“Vijana wangu wataimairisha ulinzi hapa kwa kipindi chote ambacho mzee anapatiwa matibabu”

“Nashukuru mkuu, ila ninahitaji kuzungumza na mzee mara moja”

Nikaingia ndani humu na kuwakuta madaktari wakiwa wamemtundikia mzee dripu la maji.

“Unaweza kutusubiria nje kijana”

“Hapana nina hitaji kujua hali ya mzee anaendeleaje?”

“Kwa sasa inabidi tuweze kumpumzisha kwa masaa kadhaa hapa”

“Ila anaweza kurudi kwenye hali yake ya kawaida?”

“Ndio anaweza kurudi kwenye hali yake ya kawaida. Ila tunakuomba tuendelee kuifanya kazi yetu”

Mzee Poul Mkumbo akainiita kwa ishara, nikamsogelea seheme alipo na kuninong’oneza kidogo. Akanitajia namba ya simu na kuniomba niweze kumpigia mtu huyo na kumpa maelekezo ya yeye kufika hospitalini hapa haraka iwezekanavyo. Nikatingisha kichwa kukubali ombi hili, nikatoka ndani humu na jambo la kwanza kulifanya ni kumpigia simu mtu huyo.

“Ndio”

“Mimi ni Ethan mke wa mzee Mkumbo. Ninakuhitaji uweze kufika hospitali ya KCMC amelazwa. Fanya haraka iwezekanavyo ana kuhitaji”

“Amelazwa!!?”

“Ndio”

“Sawa nipo nje ya Moshi ila baada ya masaa kidogo nitaweza kufika”

“Poa”

Nikakata simu na kumfwata RPC.

“Ninahitaji kutoka, ila nitahitaji kuhakikisha kwamba mzee anabaki salama muda wote”

“Usijali kijana ila kama huto jali ninaweza kufahamu unaelekea wapi?”

Nikamtazama RPC kwa muda kidogo.

“Ni salama hiyo sehemu, hivyo nitajilinda ila hakikisheni kwamba mzee anakuwa salama”

“Poa poa”

Nikatoka ndani humu na kutoka nje, nikamuomba dereva funguo ya gari kisha nikaondoka eneo hili na kuianza safari ya kuelekea nyumbani kwa madam raisi Tasiana Ramadhani. Sikuchukua muda sana nikafika nyumbani kwake. Ulinzi nyumbani kwake umeimarishwa tofauti na mara ya kwanza nilivyo fika nikiwa na Qeen. Gari langu likakaguliwa viruzi sana kisha nikaruhusiwa kuingia ndani ya nyumba hii ambayo kwa muda mfupi tu imebadilishwa na kuwa na muonekano wa tofauti sana. Madam raisi Tasiana akanipokea kwa furaha sana kwani toka nilipo msaidia kupata kiti cha uraisi sikuweza kuonana naye na kuzungumza naye.

“Naona kuna mabadiliko makubwa sana hapa kwako?”

“Yaa ndio hiyo nimesha kuwa raisi hakuna budi mambo kubadilika”

“Sasa kwa nini haupo ikulu, upo kwako?”

“Ni mamauzi tu, huwa nikiwa hapa kwangu nina jisikia amani sana japo sheria huwa ina nibana kuhakikisha kwamba nina kuwa ikulu. Karibu sana ndani Ethan”

“Nashukuru mama”

Tukaingia ndani kwake, tukakaa sebleni na mfanyakazi wake wa ndani akaniandalia juisi.

“Ehee sasa nimesha kabidhiwa rungu Ethan nipe mikakati wapi nianzie. Nianze na nani, Mkumbo au mwenzake kwa maana kila siku huwa nina waota kila nikilala. Natamani sana kuwafumua fumua, hembu niambie mwanangu yupi tumuangushe?”

Madam raisi Tasiana Ramadhani alizungumza kwa shauku kubwa huku akinitazama usoni mwangu. Taratibu nikashusha pumzi huku nikimtazama na moja kwa moja akilini mwangu nikamuwaza mzee Mkumbo kwanikwa kile alicho kutana nacho leo nina imani kwamba hakijamtosha na ninahitaji aweze kukutana na kikubwa zaidi ya hili la leo asubuhi.



ENDLEA

“Ethna mbona kimya hunijubu?”

“Nafikiria mama yangu kwa maana kila mmoja tunatakiwa tumuanze kwa akili kwa maana tukiende hivi hivi tunaweza kupoteza ushahidi wote kwao”

“Ni kweli ila kwa sas animeunda timu ya wapelekezi makini sana ambao wanaweza kuifanya kazi hiyo kikamilifu na nina imani kwamba hakuto kuwa na hata mmoja ambaye ataweza kuepuka katika mkono wangu”

“Ni vizuri mama ila anza na huyu mpinzani?”

“Kwa nini ikiwa adui namba moja unatembea naye na unakaa naye karibu?”

“Hivi sasa nina jukumu moja la kumuathiri kisaikolojia?”

“Kivipi?”

“Unajua katika vita ya ya kumuangusha mtu, hususani yule anaye jihisi kwamba ana manguvu mengi sana. Nilazima uhakikieshe kwamba una mla taratibu taratibu, akifikia hatua ya kuanguka basi ni moja ya ushindi mkubwa sana ambao mtu unaupata kwani hato weze kunyanyuka tena kwenye maisha yake”

“Ni kweli hilo ni jambo zuri ila nahisi kama linachukua muda mrefu sana?”

“Mama nipo kwenye hatua nzuri kwa sasa, kuna mengi sana ambayo nimeanza kuyafahamu juu ya huyu mzee”

“Nani?”

“Mkumbo”

“Ehee niambie una muathiri vipi kisaikolojia?”

Nikamtazama madam raisi Tasiana.

“Kwasasa mama yangu ni ngumu sana kuweza kukueleza. Unajua mimi ni mtu ambaye napanda nifanye mipango yangu ikikamilika ndio nina zungumza. Siku ile laiti kama ningekuja hapa mikono mitupu na kuzungumza na wewe nina imani kwamba ungenikatalia kila jamboa mbalo ningelizungumza si kweli?”

“Kweli, kwani pia sikuweza kukuamini kwa haraka sana hadi pale nilipo tangazwa kuwa raisi wa hii nchi”

“Basi nipe muda kw amzee Mkumbo ila hao wengine hakikisha kwamba una shuhulika nao kikamilifu na endapo itatokea utahitaji msaada wangu. Nipo tayari kukusaidia mama yangu”

“Nashukuru sana Ethan. Unajua nimekuwa najiona ni mwanamke mwenye bahati sana kukutana na wewe kijana. Nina imani kwmaba Mungu ana makusudi nasi”

“Ni kweli mama yangu”

Nilizungumza huku nikiyakumbuka maneno ya Ethna aliyo nisisitizia kwamba madam raisi Tasiana atakaa madarakani kwa miaka michache sana ili niweze kumfanikisha aendelee kukaa madarakani kwa miaka mingi sana inabidi niweze kumua mwanaye na kuachana na Camila pamoja na Biyanka.

“Mama hivi mwanao yupo wapi, toka nimekuja sijaweza pata nafasi ya kuweza kukutana naye”

“Yaaa Hawa ameondoka amekwenda Marekani kuna baadhi ya mambo nimeweza kumuagiza, si unatambua ni mwana sheria hivyo kuna maswala anatakiwa kuyaweka sawa”

“Sawa mama yangu, atarudi lini?”

“Next weak ni jana tu nilizungumza naye akakukumbuka na kuomba namba yako anaweza kukupigia muda wowote”

“Sawa mama yangu. Naomba ruhusa yako niweze kurudi hospitalini ili niweze kuwa pamoja na mzee”

“Hivi anasumbuliwa na nini?”

“Yaani ni presha tu hakuna kingine si unatambu kwamba waliweka mategemeo makubwa sana na mambo yamekuwa mambo”

“Hahaaa…eheee Ethan ngoja kwanza mwanangu hembu naomba uniambie nini siri ya ushindi wangu. Kwa maana sikutarajia kabisa kwenye ushindano huu niibuke kidedea?”

“Ni mambo ya IT. Ila siku nikiwa na nafasi kubwa mama yangu nitakuelezea kila jambo. Naomba sasa niweze kuondoka”

“Sawa mwanangu. Mimi nipo pamoja nawe. Halafu unaweza kunisaidia wafanya biashara waaminifu waweze kuwekeza katika nchi hii?”

“Hilo ni jambo rahisi, hata mimi nitaendelea kuwekeza katika nchi yangu. Ila weka mambo sawa, zoea ofisi yako na hakikisha kwamba wawekezaji wakifika hapa hawakutani na mamo magumu”

“Nimekuelewa mwanangu.”

“Kuna jambo moja nimelisahau mama yangu. Ninaomba uweze kunipatia eneo nina hitaji kujenga uwanja wa kisasa wa timu yangu ambayo nitaianzisha hivi karibuni”

“Woooo ni wewe tu. Unaonaje uwanja huo ukaujengea hapa mkoni Moshi kwa maana kuna maeneo mengi mazuri na hii hali ya hewa ni nzuri sana na isitoshe mkoa wangu upo safi sana”

“Usijali mama yangu. Nitajaribu kuzungumza na wakandarasi ili waje mkoani hapa na kama watafanikiwa kupima na kuona kwamba tunaweza kujenga kiwanja basi bahati itangukia kwenye mkoa wetu mama yangu”

“Nashukuru sana mwanangu. Mungu akubariki sana. Nikizungumza na wewe huwa nina jisikia amani sana, tofauti na ninavyo zungumza na watu wengine”

“Usijali mama yangu. Mimi ni mwanao tu na nitahakikisha nina ishi kwenye utaratibu mzuri wa kufwata sheria za nchi, nisije kujiona nina juana na raisi na nikaisha katika maisha ya unyanyasaji”

“Ni kweli mwamangu, kuna watu ukijuana nao basi wanaishi kwneye misha ya kujigamba”

“Sawa mama yangu”

Tukaagana na madam raisi Tasiana. Nikaingia ndani ya gari na kuanza safari ya kurudi hospitalini, nikafika hospitalini salama, na kukuta ulinzi wa askari ukiwa umeimarishwa. Moja kwa moja nikaelekea hadi eneo la chumba cha mzee Poul Mkumbo na kuwakuta askari wakiwa wameongezeka na kuwa wanne huku mkuu wao akiwa hayupo eneo hili.

“Mzee bado yupo ndani ya hichi chumba?”

“Ndio”

Nikafungua mlango, nikastuka sana mara baada ya kumkuta mmoja ya watu walio husika katika kuwaua wazazi wangu akiwa amesimama pembeni ya kitanda cha mzee Poul Mkumbo huku wakionekana wakizungumza mazungumzo muhimu sana.

“Ethan nitakuita”

Mzee Poul Mkumbo alizungumza kwa upole huku akinitazama usoni mwangu. Nikatoka chumbani humu huku nikiwa nimejawa na gadhabu ambayo ninazidi kuizuia kuhakikisha kwamba hakuna mtu anaweza kuiona. Nikakaa nje ya chumba hichi kwa zaidi ya dakika ishirini, mwanaume huyo akatoka, hakunisalimia zaidi ya kuondoka eneo hili kwa mwendo wa kujiamini sana. Nikaingia chumbani humu na kumkuta mzee Poul Mkumbo akijitahidi kukaa kitandani.

“Inabidi tuondoke”

Mzee Poul Mkumbo alizungumza huku akijichomoa sindano ya dripu iliyo mchoma mkononi mwake.

“Mbona dripu halijaisha?”

“Muda wa kukaa hapa ni mdogo na sina usalama wa uhakika, ninahitaji kuondoka sasa”

Mzee Poul Mkumbo akashuka kitandani, nikatamani kumuuliza huyu aliye weza kufika hapa ni nani ila nikajizuia. Tukatoka ndani humu, tukakutana na daktari kwenye kordo.

“Muheshimiwa vipi mbona unaondoka kabla ya muda?”

“Sina muda wa kuendelea kukaa hapa hospitali”

“Ila mzee bado hali yako haijawa sawa”

“Nitakuwa sawa mbele ya safari”

Mzee Poul Mkumbo alizungumza kwa kujiamini, tukaingia ndani ya gari na kuondoka hospitalini hapa na kuwaacha baadhi ya wagonjwa na wahudumu wa hii hospitali wakishangaa. Gari mbili za polisi zikaendelea kusindikiza hadi uwanja wa ndege. Tukapanda ndege ya kukodisha na kuianza safari ya kurudi jijini Dar es Salaam. Ukimya ukatawala ndani ya ndege huku mzee Poul Mkumbo akionekana akiwa amejawa na mawazo mengi sana.

“Mzee”

Nilimuita mzee Poul Mkumbo, taratibu akanitazama.

“Unajisikiaje?”

“Natafakari haya mauza uza niliyo yaona leo. Yaani na utu uzima wangu huu, ninajikoleaa aha…Hapana aisee lazima nifanya jambo”

Nikajikuta nikicheka kimoyo moyo kwa maana mzee Poul Mkumbo amekuwa mnyonge sana, kiasi cha kupoteza hata nuru nzuri ya uso wake.

“Unahitaji kufanya nini mzee?”

“Nimeagiza mtaalamu kutoka Mombasa Kenya, sasa hivi anaelekea Dar es Salaam. Lazima afaye jambo”

“Mtaalamu, sijaukuelewa hapo mzee?”

Mzee Poul Mkumbo akanitazama kwa jicho kali.

“Ni mganda”

Mzee Poul Mkumbo alilinijubu kwa umsisitizo ila kwa ufupi. Sikuhitaji kuzungumza kitu chochote zaidi ya kukaa kimya. Tukafika jijini Dar es Salaam na kukuta walinzi wake uwanja wa ndege, tukaingia kwenye gari na kuondoka.

“Munaweza kunipitisha ofisini kwangu”

Nilimuambia Mzee Poul Mkumbo huku nikimtazama usoni.

“Dereva badilisheni msafara, tumpitishe kijana ofisini kwake”

Mzee Poul Mkumbo na madereva hawa wa gari zote zatu wakawasiliana kwa vinasa sauti maalumu kisha gari zote tatu zikageuzwa na safari ya kuelekea ofisini kwangu ikaanza.

“Ethan”

“Ndio mzee”

“Kila jambo lililo tokea hakikisha kwamba humuambii Biyanka wala mke wangu. Sawa?”

“Sawa mzee”

Tukafika ofisini kwangu nikashuka kwenye gari kisha mzee Mkumbo akaendelea na safari ya kueleeka nyumbani. Nikasalimiana na wafanyakazi wangu na moja kwa moja nikaelekea ofisini kwangu kwani nina muda kidogo sijafika ofisini hapa.

“Kuan lipi jipya?”

Nilimuuliza sekretari wangu.

“Kuna baadhi ya mikataba ipo mezani kwako muheshimiwa”

“Sawa”

Nikaingia ofisini kwangu na kuanza kupitia mafaili yote yaliyopo mezani mwangu na kuyafanyia kazi kikamilifu.

“Mganga wake amesha fika”

Niliisikia sauti ya Ethan nyuma yangu na nikajikuta nikistuka sana huku nikigeuka.

“Unastuka stuka nini, miaka yote hiyo hujanizoea?”

“Si kwa kunitokea nyuma, nina stuka kumbuka mimi ni binadamu”

“Okay tuyaache hayo. Mganga wa mzee wako amesha fika”

“Ni mganga mzuri?”

“Ni mzuri ila hana uwezo wa kushindana na mimi”

“Mmmm asije akafumbua mambo yote niliyo mfanyia mzee Mkumbo”

“Niamini hawezi kufanya jambo lolote”

“Mmmm umejipangaje kwa mafano ukakaribia karibia kidogo kuhisi kwamba mimi ndio muhusika?”

“Wewe subiria. Utaona, baadae”

Ethan akapote ofisini kwangu. Simu yangu ikaanza kuita, nikatoa mfukoni na kukuta namba mpya inanipigia katika mtandao wa Whatsapp video. Nikaitazama kwa muda kidogo kisha nikaipokea na kuiweka mbele yangu. Nikakutana na sura ya Hawa akiwa emelala kitandani huku akiwa amevaa earphone masikioni mwake.

“Ethan mambo”

“Poa za kwako?”

“Safi, samahani kwa kukupigia muda huu”

“Usijali, vipi huko ni usiku?”

“Yaaa huku ni usiku mpendwa. Upo ofisini?”

“Ndio. Vipi Marekani?”

“Mungu anasaidia. Nilihitaji kukusalimia na hii ndio namba yangu”

“Nashukuru kuipata. Kuna mambo nina yafanya ninaomba tuwasiliane baadae”

“Ohoo sawa usijali”

Nikakata simu na kutoka ofisini kwangu, nikamkabidhi sekretari mfaili niliyo yafanyia kazi nikatoka nje ya ofisi hii na kumuomba dereva wa kampuni kunipelekea nyumbani kwa mzee Poul Mkumbo. Nikafika nyumbani kwa mzee Mkumbo na nikashuka getini na dereva akaondoka, moja kw amoja nikaingia ndani bila ya kukaguliwa na walinzi. Nikwia nikakaribia mlangoni nikaanza kusikia ngoma ikipigwa pigwa, nikafungua mlango huu wa sebleni na kukuana na moshi mwingi sana ulio samaba sebleni kote. Nikamkuta mzee Poul Mkumbo akiwa amekaa chini katika shuka jekundu.

“HUYU HAPAAAAA”

Nikastuka sana mara baada ya mganga kuzungumza kwa nguvu huku akininyooshea kidole chake huku akitetemeka mwili mzima jambo lililo wafanya Mzee Poul Mkumbo, Biyanka na mama Biyanka wakinitazama kwa mshangao sana.



Macho yakanitoka, mapigo ya moyo yakaanza kunienda kasi, nikatamani kupiga hatua kadhaa nyuma ili nikimbie ila nikahisi miguu yote ikiwa imeshiwa na nguvu kabisa, kwani kwa hili alilo lifanya huyu mganga kwa kweli lina niogopesha.

“Huyo kijana ndio ngao kubwa ya familia yako isianguke. Ila kama si yeye sasa hivi mzee wangu unekuwa umesha filisikaa. Hahahaaaaa”

Mganga huyu alizungumza maneno ambayo yakanifanya nishushe pumzi nyingi sana huku nikimkazia macho. Mwili taratibu ukaanza kurudi kwenye hali yake ya kawaida, taratibu Biyanka akanifwata hadi sehemu hii nilipo na kunishika mkono. Tukasogea kimya kimya hadi alipo kaa mama Biyanka kwenye sofa kubwa la hapa sebleni. Mganga nyu akendelea kupiga piga vingoma vyake viwili ambavyo vinatoa mlio mkali sana.

“Usiogope mume wangu”

Biyanka alizungumza kwa sauti ya chini huku akininong’oneza sikioni mwangu. Nikatingisha kichwa nikimaanisha kwamba nina msikia. Mganga huyu akaanza kumzunguka zunguka mzee Mkumbo huku akimpiga piga na mkia wa farasi kichwani mwake.

“Ninaona giza”

Mganga alizungumza huku sote tukishangaa jinsi taa za sebleni hapa zilivyo na mwanga mkali sana.

“Naona GIZZZAAAAAAA……”

Mganga huyu aliongeza sauti yake kwa kuzungumza, akauachia unyoya wake na kuutupa chini, akaanza kuyafikicha macho yake na kutufanya watu wote tuendelee kumshangaa.

“Sioni mzee wangu”

“Heee!!?”

Mzee Poul Mkumbo alikurupuka chini alipo kaa na kumtazama mtaalamu wake huyu ambaye anaendelea kufikicha macho yake mithili ya mtu aliye ingiwa na povu la sabuni machoni wakati wa kuoga.

“Huoni nini sasa, maadui zangu au Live Live?”

“Live mzee…..Ohoo kichwa changu kinaniuma…..Ohoo nisaidieniiii nakufaa mimi”

Mganga alizungumza huku akilia, sote tukasimama huku kila mmoja akiwa amejawa na wasiwasi. Mganga akaanza kujibamiza bamiza kwenye masofa na kutufanya tumkwepe kwani vikumbo vyake vina nguvu sana.

“Hembu iteni hao walinzi”

Nikatoka kwa haraka na kuwaita walinzi, kwa haraka wakaingia ndani hapa. Kila mmoja akabaki akiwa amejawa na mshangao mkubwa sana kwani jinsi mganga alivyo lala hapa chini na kuitupa tupa miguu yake amekuwa ni kama mtu anaye uwawa kilazima kwa kutumia mto.

“Munashangaa nini hembu mshikeni huyu mtu?”

Mzee Poul Mkumbo alizungumza kwa kufoka, kitendo cha walinz wake kupiga hatua moja kumsogelea mganga huyu. Mganga akapiga ukelele mmoja mkali sana na macho yakamtoka nje na kumpasuka mithili ya ftuza linavyo banjika.

Si mlinzi, si mzee Mkumbo wala sisi kila mmoja akajitafutia njia yake ya kukimbilia. Mimi na mama mkwe tukajikuta tukiwa jikoni kwa pamoja huku kila mmoja akihema kwa woga kwani sidhani kama kuna mtu amewahi kushuhudia tukio la kutisha kama hili.

“Ohoo Mungu wa Yakobo. Tukimbilie wapi sisi, tumekutenda maovu sana na unaamua kutulipa hapa hapa duniani”

Mama mke walizungumza huku akiwa amepiga magoti yake chini na kunyoosha mikono yake yote miwili juu ikiwa ni ishara ya kusali.

“Bwana Yesu, tusamehee sisi ohoo Mungu wangu”

Tukasikia mzinga mwengine mzito ulio mfanya maam Biyanka kukatisha maombi yake na kunikimbilia sehemu nilipo simama na kunikumbatia huku mwili wake wote ukimtetemeka.

“Ni nini hicho Ethan?”

“Hata mimi sifahamu mama”

Taratibu nikaitoa mikono ya mama mkwe mwilini mwangu, kisha taratibu nikaanza kunyata kuelekea sebleni. Mwili mzima ukahisi kama umepigwa shoti kwani kichwa cha mganga huyu kimepasuka na ubongo wote upo nje.

‘Hata wewe unaogopa?’

Niliisikia sauti ya Ethan ndani ya nafsi yangu.

‘Wewe ndio umefanya haya yote?’

‘Ndio’

‘Kwa nini?’

‘Nilikuambia ngoja uone. Nimedhibitisha kile nilicho kueleza na laiti kama ingewa si kubadilisha maneno huyo mpuuzi hapo chini basi angeenda kufunguka kila kitu’

‘Weee unataka kuniambia……’

‘Alihitaji kukutaja wewe kama adui wa hii familia, ila kwa haraka niliweza kubadilisha kinywa chake’

‘Sasa inakuwaje na huyu sasa?’

‘Hapo hakuna cha kufanyaje, iteni polisi waje kuchukua mzoga wao’

Walinzi wawili wakaingia ndani humu huku wakiwa na bastola mikononi mwao. Wote wakabaki wakiwa wamejawa na mshangao.

“Ohoo MUNGU wangu!!”

Mlinzi mmoja alizungumza huku akiendelea kuishikilia bastola yake vizuri sana. Mzee Poul Mkumbo na walinzi wake wengine wawili wakaingia hapa sebleni, mzee Mkumbo akabaki ameziba mdomo wake kwa mshangao mkubw asana.

‘Kuendelea kumuathiri kisaikolojia huyo chini wako ni jambo muhimu sana, sasa tukiingia kwenye maliza zake basi tutahakikisha tunamuacha na nguo zake tu alizo zivaa”

Niliendelea kuisikia sauti ya Ethan huku nikiwashuhudia walinzi hawa akijikaza kiujasiri na kumsogelea mwili wa mganga huyu ambao tayari kwa sasa ni maiti. Nikamuona mama mkwe akitoka katika mlango wa jikoni, kwa ishara ya mkono nikamzuia asifika sebleni hapa, kwani nina fahamu ana presha. Mama mkwe akanielewa huku uso wake ukionekana kujawa shauku ya kuhitaji kufahamu ni nini haswa kimetokea. Nimashuhudia Biyanka akishuka kwenye ngazi za gorofani taratibu taratibu huku akiwa makini sana.

“Baby what’s goin on?”(Mpenzi ni nini kinacho endelea?)

Biyanka aliuliza kwa sauti ya woga.

“Musifike hapa sebleni”

Mzee Poul Mkumbo alizungumza kwa sauti ya juu ya na kujiamini sana.

“Baba kwa nini?”

“Nimesema hivyo kila mmoja arudi sehemu alipo kuwa. Sio ombi ni amri”

Mama Biyanka wakaungana na mwanaye na kupandisha gorofani pasipo kuushuhudia mwili wa marehemu jinsi unavyo endelea. Nikasogea eneo la karibu la mwili huu.

“Hembu waulizeni hao polisi wamefika wapi?”

Mzee Poul Mkumbo alitoa maagizo hayo kwa mmoja wa walinzi wake na akafanya hivo kama alivyo ambiwa.

“Wanakaribia hapo getini”

“Sawa”

Baada ya dakika kama mbili tukasikia ving’ora vya gari za polisi. Walinzi wawili wakatoka nje na walipo rejea ndani, wakawa wameongozana na askari sita wenye silaha. Kila askari aliye ona maiti ya mganga huyu akabaki akiwa na mshangao.

“Habri yako mkuu”

“Sio nzuri, kama unavyo jionea huyu mtaalamu amenifia hapa kwangu”

“Ahah…..imekuwaje?”

“Hata mimi sielewi, yaani alianza kulalama macho yanamuuma, mara haoni baada ya muda kidogo macho yakampasuka. Watu wote hapa tukatawanyika hapa sebeleni, tukiwa katika sehemu tulizo kimbilia tukasikia mpasuko wa kichwa chake na hapo ndipo stori ilipo ishia”

“Mmmmm yaani, sijapata picha halisi kabisa muheshimiwa”

“Aisee nimetoa maelezo yaliyo nyooka. Chukueni maiti muipeleke Muhimbili, huku nikifanya taratibu za kuipelekea nchini Kenya kwa mazishi kwa maana huyu si Mtanzania”

“Sawa ila inabidi tufanye uchunguzi kabla ya kuichukua maiti”

“Uchunguzi gani, ina maana kwamba hamuamini nilicho sema au?”

“Polisi huwa hatuamni maneno matupu hadi tuweze kutendea kazi kile tunacho hitaji kukifanyia kazi muheshimiwa”

Askari huyu alizungumza kwa busara na kujiamini. Hakujali kama mzee Poul Mkumbo ni mtu mkubwa sana hapa nchini, ila akasimamia katika misingi ya kazi yake inavyo hitaji. Akawapa ruhusu vijana wake kuanza kufanya upelezi, ambazo kila mtu hapa aliweza kuhojiwa kwa jinsi anavyo weza kushuhudia tukio hilo. Biyanka na mama mkwe nao wakaohojiwa katika muda na wakati tofauti tofauti. Walipo jiridhisha wakachukua mwili wa marehemu na kuondoka nao.

Hapakuwa na mtu ambaye aliweza kudhubutu hata kukilalia kitanda chake, woga ukatawala katika familia hii, japo kwa upande wangu kidogo nina amani kwani nina fahamu ni kitu gani kinacho endelea.

“Mama mimi kesho ninarudi kwangu. Nimechoka na mambo haya”

“Tunakwenda wote mwanangu”

“Hakuna mtu kuondoka nyumbani hapa”

“Baba hapana, ninaondoka. Nina kwangu na nina maisha yangu. Mambo ya kuja kushuhudia mambo ya ajabu ajabu kama haya. Haki ya Mungu baba nimechoka”

Biyanka alilalama sana huku akimkazia macho baba yake.

“Kama ingekuwa sio mimi usinge kuwa na maisha hayo. Mimi ni baba yako na nitaendelea kuwa baba yako hivyo funga bakuli lako. Mutakaa hapa na sitaki ujinga. Unapenda wakati wara, shida unakimbia si ndio?”

Mzee Mkumbo alimkoromea Biyanka na kumfanya awe mpole.

“Sitaki ujinga mimi”

Mzee Mkumbo aliendelea kulalama huku akiachia misunyo isiyo na idai.

“Ethan”

“Ndio mzee”

“Kesho utaamkia Muhimbili kufwatilia mwili wa huyu boya”

“Mume wangu, sasa hii imezidi. Kumbuka mtoto wa watu hapa ana kaa kwa ajilia ya dhamana ya mwanetu. Ana mambo yake ya kufanya, si kila jambo afanye yeye hembu kuwa na kipimo cha kumuachia maagizo basi”

Maneno ya mama mkwe yakamfanya mzee Poul Mkumbo kumtazama kwa jicho kali la hasira kisha akaachia msunyo mkubwa zaidi ya mishunyo mingine yote.

“Hata ukinisunya ila ukweli ndio nimesha kuambia”

“Mama Biyanka funga kinywa chako. Nitakuvuruga sasa hivi”

Mzee Mkumbo alizungumza kwa kukoroma.

“Nivuruge ila ukweli nimekuambia”

Mama Biyanka akajikaza kumpandishia mzee Mkumbo.

“Wewe mwanamke, umenisahau eheeee?”

“Nakujua vizuri. Mwanaume una roho mbaya, chafu. Roho ya kinyama ndio maana Mungu anakudhihirishia kwamba wewe ni mtu mbaya, ndio maana kila unacho kifanya hakiendi”

Mama mkwe alilalama huku machozi yakimwagika usoni mwake. Nikamshuhudia mzee Mkumbo akikunja mikono yake ngumi huku mwili mzima ukimtetemeka kwa hasira.

“Ethan kesho hakuna kwenda popote”

“NYAMAZAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAA……………………..”

Mzee Poul Mkumbo alizungumza kwa sauti ya ukali iliyo tufanya mimi na Biyanka tumuogope.

“Hata ukipayuka kwa makelele yako unahisi kwamba nitakuogopa eheee?”

Mama alizungumza huku akimtazama mzee Mkumbo. Mzee Mkumbo akasimama kutoka sehemu alipo kaa na kuanza kumfwata mama hapa alipo kaa nasi. Mama mkwe akanyanyuka huku akijifunga tenge lake vizuri, akijianda kwa chochote kile ambacho kinakwenda kumtokea.

“Nitakuua wewe mwanamke”

Mzee Mkumbo alizungumza huku akimuwahi kumshika mama koo lake na kuanza kuliminya. Kabla hata hatujasimama kuamua ugomvi huu. Mama mkwe akampiga teke mzee Mkumbo eneo la sehemu za siri na kumfanya mzee Mkumbo amuachie huku akianguka chini na kutoa mngurumo wa maumivu makali sana aliyo yapata.

“Unahisi kwamba kila siku nina weza uwa mnyonge kwako eheee?”

Mama mkwe alizungumza huku akimsindikizia mzee Mkumbo teke jengine la tumboni.

“Mama jamani, munafanya nini. Muna niabisha mbele ya mume wangu”

“Acha nimfunze adubu mshenzi huyu. Amezoea kila siku kuniana mimi mnyonge tu”

Mama alizungumza huku akilia kwa uchungu sana.

“Biyanka mpeleke mama chumbani”

“Ethan baba yangu wewe niache tu. Nataka kumshuhulikia huyu mjinga. Ni mambo mangapi nimekufanyia kwenye maisha yako wewe mwanaume. Ni siri ngapi ambazo nimekutunzia wewe eheee?”

Mama mkwe alizungumza kwa ukali huku akiwa amemuinamia mzee Poul Mkumbo anaye endelea kuugulia maumivu ya sehemu zake za siri kwani kwa teke alilo pewa si la mchezo mchezo, hata uwe jasiri vipi ni lazima ukubali kuwa mnyonge kwa muda kadhaa.

“Mama Biyanka nikinyanyuka hapa haki ya Mungu nitakuua”

“Umuue nani eheee. Umuue nani. Umenisahau si ndio?”

Mama mkwe akamtandika kofi zito mzee Mkumbo usoni mwake. Mzee Mkumbo akajaribu kunyanyuka kutoka chini hapa alipo anguka, ila mama mkwe akamuwahi kumuwekea kigoti cha mguu wa kulia kifuani mwake na kumzuia vizuri sana.

“Wewe unataka kwenda wapi?”

Mama mkwe alizungumza huku akimshindilia mzee Poul Mkumbo ngumi nyingine ya usoni. Nikamtupia jicho Biyanka sehemu aliyo kaa. Masiki ya Mungu ameshikwa na bumbuwazi pana sana, hajui ni nini atafanya, hajui aanzie wapi kuwazuia wazazi wake, mdomo wake dhairi unaonyesha unahitaji kuzungumza jambo ila ana shindwa na mbaya zaidi walinzi wote wapo nje wakiendelea kuimarisha ulinzi wa nyumba hii.

“Leo utanijua mimi ni nani. Kama ulinikuta nikiwa mwana jeshi basi usihihi kwamba nimesahau mbinu zote za kijeshi mjinga wewe”

Mama mkwe alizungumza huku akiendelea kuachia vitasa mfululizo usoni mwa mzee Mkumbo.

‘Kumbe mama alikuwa ni mwanajeshi?’

Nilijiuliza swali hili huku nikiendelea kumshuhudia mzee Mkumbo akipokea dhuluba hii kutoka kwa mke wake.

“Nikuue wewe mjinga, usiye weza hata kuotesha mbegu tumboni mwa mwanamke?”

Kauli hii tata, ikatufanya mimi na Biyanka tustuke sana. Hata mzee Poul Mkumbo japo yupo kwenye dhuruba kali ila naye akastuka.

“Unastuka nini? Unahisi kwa madhambi yako hayo ungeweza kunipa ujauzito? Sasa ni hivi Biyanka sio mwanao wa damu na kuanizia leo sahau kama ulisha wahi kuwa na mwanamke kama mimi wala mtoto kama Biyanka.”

Mama mkwe mara baada ya kumaliza kuzungumza hivyo akamuachia mzee Poul Mkumbo na kuondoka katika seble hii ndogo na kutacha watu wote tukiwa tumejawa na mshangao mkubwa sana.



Mzee Mkumbo akajitahidi kunyanyuka ila akashindwa. Biyanka akabaki akitetemeka kwani ukweli huu ulio zungumzwa na mama nina imani umemuweka katika hali tete. Tukamuona mama akitoka ndani huku akiwa na begi kubwa la nguo. Nikamkimbilia hadi sehemu mama alipo.

“Mama tafadhali nina kuomba usifanye hilo unalo taka kufanya”

“Ethan, nina kuheshimu mwanangu. Nakuomba upishe”

“Mama”

“Ethan tafadhali nina kuomba upishe njia”

Mama alizungumza kwa ukali, nikasogea pembeni na akaanza kuburuta begi lake kuelekea nje. Biyanka akanyanyuka na kumkimbilia mama nje huku nami nikimfwata mzee Poul Mkumbo sehemu alipo lala na kuanza kumsaidia kumnyanyua.

“Pumbavu nitamuua huyu mwanamke”

Baba mkwe alijibaragazua huku akiwa amezishika sehemu zake za siri. Ila ukweli ni kwamba leo amepatikana. Ukimya ukatawala hapa sebleni huku mzee Mkumbo akiendelea kuugulia kwa maumivu.

“Nenda kamzuie mama yako”

Mzee Mkumbo alizungumza kwa sauti ya upole na unyonge. Nikasimama na kutoka nje, nikamkuta mama akiwa amekumbatia na Biyanka huku walinzi wawili wa kike wakiwa wamesimama pembeni ya gari ambalo mara nyini huwa ana litumia mama mkwe kwenye matembezi yake. Nikawasogelea sehemu walipo, wakaachiana taartibu na mama akanikumbatia na mimi huku akimwagikwa na machozi.

“Ethan”

“Naam”

“Naam”

“Nakuomba uweze kumlinda mwanangu sawa”

“Sawa mama”

“Hakikisha kwamba anaishi salama, hakikisha kwamba hakumbwi na matatizo ya aina yoyote sawa baba”

“Sawa mama”

“Kwaherini”

Mama akaniachia kisha akafunguliwa mlango wa gari na mlinzi wake, wakaingia kwenye gari na taratibu wakaanza kuondoka. Biyanka akanikumbatia huku akiangua kilio kikubwa sana, nikaanza kumbembeleza kwani hili tukio lililo tokea leo ni kubwa sana kwenye maisha yake.

“Tuondoke mume wangu”

“Twende wapi?”

“Sijui ila tundoke”

Biyanka alizungumza huku akiniachia, akaanza kutembea kueleka ndani, tukakutana na mzee Mkumbo mlangoni, akampiga kikumbo mzee Mkumbo na kukimbilia ndani.

“Vipi?”

“Mama ameondoka”

“Ohoo amekwenda wapi?”

“Sijajua kabisa amekwenda wapi”

“Nitajua ni wapi kwa ku…..”

Mzee Mkumbo hakuimalizia sentensi yake mara baada ya kumuona Biyanka akiburuza begi lake.

“Unakwenda wapi mwanangu”

Mzee Mkumbo alizungumza kwa woga mkubwa sana.

“Biyanka mwanangu”

“Weeeee. Uneharibu maisha ya mama yangu na yangu niache”

“Biyanka mama yako zile ni hasira tu, wewe ni mwanangu. Wewe ni damu yangu huna baba mwengine tofauti na mimi”

Mzee Mkumbo alijaribu kuzungumza huku akimshika Biyanka mkono ila Biyanka kwa hasira akautoa mkono wa baba yake.

“Ninaondoka usinitafute. Ethan twende”

Biyanka akanishika mkono na tukatoka eneo hili na kuanza kuelekea kwenye gari langu. Akafungua mlango wa nyuma wa gari hii na kuingiza begi lake kisha akafunga kwa nguvu. Akaingia upande wa dereva na kuwasha gari.

“Biyanka tambua nina kupenda sana mwanangu. Tambua kwamba wewe ndio kipenzi changu”

Mzee Mkumbo alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake. Biyanka hakujali hilo, nikamtazama mzee Poul Mkumbo kwa huruma sana kwani kila siku anakutana na janga kubwa. Nikafungua mlango wa gari na kupanda.

“Mke wangu unaweza kumsikiliza baba kidogo”

“Ethan sihitaji kusikia chochote bwana. Kama unampenda sana huyo mzee shuka kwenye gari niondoke mwenyewe”

Biyanka alizungumza kwa ukali sana huku tukianza kuondoka eneo hili. Kutokana lengo langu kubwa kwa mzee Poul Mkumbo ni kumpokonya kila kitu anacho kipenda, hivyo kazi yangu inazidi kufanikiwa, kwani kama ni uraisi amekosa, mke kwa sasa amekosa na mtoto pia amekosa. Kilicho baki ni kumkosesha mali zake zote anazo zitarajia. Geti likafunguliwa na Biyanka akaanza kuendesha gari hili kwa mwendo wa kasi sana.

“Endesha vizuri”

“Usinifundishe”

“Nisikufundishe nini?”

“Kwani hapa nini fanya nini?”

Nikamtazama Biyanka kwa macho makali sana ila kazidi kuongeza mwendo kasi wa hili gari.

“Biyanka punguza mwendo”

“Sipunguzi”

“Unataka tufe eheee?”

Nilimuuliza Biyanka kwa ukali huku nikitazama jinsi spidi mita inavyo zidi kuongezeka. Nikaufunga mkanda wa siti yangu taratibu kwani hata likijitokeza la kujitokeza basi sinto pata madhara makubwa. Tukafika kwenye moja ya fukwe za bahari na Biyanka akasimamisha gari, akafungua mlango na kushuka na kuanza kukimbia mithili ya mtu aliye changanyikiwa.

Nami nikashuka kwenye gari na kuanza kumkimbiza. Nikafanikiwa kumdaka kiunoni mwake na kwa nguvu zake zalio jitahidi kunitoa mikono yangu ili niweze kumuachia, tukajikuta tukianguka chini kwenye huu mchanga mwingi sana.

“Unafanya nini Biyanka”

“Ethan acha nife, acha nife sina faida ya kuendelea kuwepo hapa duniani”

Biyanka alizungumza huku akijitahidi kunyanyuka ila nikamzuia. Uzuri mambo haya yote yanatokea wakati huu wa usiku.

“Acha ujinga, unataka kujiau kisa nini eheee? Nani amekuambia kwamba wewe huna faida eheee”

Nilizungumza huku nikimtazama Biyanka kwa ukali sana.

“Kama umekosa upendo kutoka kwa baba yako au wazazi wako. Mimi nina kupenda, ndio maana hadi leo hii nipo na familia yako, matatizo yako ni yangu, sasa kwa nini unaniletea ujinga eheee”

Biyanka akakosa cha kujibu na kuendelea kulia kwa uchungu sana.

“Nyanyua twende nyumbani”

“Ethan siendi popote. Hembu niache nikae hapa mwenyewe”

“Siwezi kukuacha kijinga jinga. Kama unahitaji nikutie vibao, wewe endelea kuniletea ujinga. Nyanyuka”

Nilizungumza kwa ukali na Biyanka akanyanyuka taratibu huku akinitazama kwa wasiwasi. Tukarudi sehemu lilipo gari letu, tukaingia ndani ya gari na kuondoka eneo hili huku mimi nikiwa ndio dereva. Tukaondoka jijini Dar es Salaam na kuelekea katika mji wa Bagamoyo. Tukafika kwenye hoteli ambayo mara nyingi nikija kwenye mji huu wa Bagamoyo. Nikachukua kiasi kidogo cha pesa kilichopo ndani ya gari langu na tukashuka.

Tukafika mapokezi na kumkuta kijana mmoja.

“Karibu”

“Asanteni. Vyumba vipo?”

“Ndio muheshimiwa vyumba vipo”

“Vyenye hadhi ya VIP vipo?”

“Ndio muheshimiwa”

Nikafanya malipo ya siku mbili, tukaandikisha majina yetu na kukabidhiwa kadi maalumu ya kufulia mlango na kuelekea kilipo chumba chetu. Tukaingia ndani na Biyanka moja kwa moja akapitiliza hadi kitandani na kujilaza.

“Amka tukaoge, tuna michanga mingi”

“Niache nipumzike”

“Mke wangu”

“Ethan sipo sawa, nimekuheshimu kwa sababu nina kupenda ila nisinge weza kufika hata hapa hotelini niache bwana”

Nikamtazama Biyanka kwa sekunde kadhaa kisha nikelekea bafuni. Nikaanza kuoga taratibu huku nikiendelea kujipongeza kwa kazi nzuri ambayo ninazidi kusambaratisha familia ya mzee Poul Mkumbo. Nikarudi chumbani huku nikiwa nimejifunga taulo kiunoni mwangu. Kwa jinsi Biyanka alivyo lala kwa kifudifuni na kusababisha makalio yake kujenga kimuinoko ambacho mwanaume yoyote akimuona ni lazima atamtamani. Nikamsogelea Biyanka na kumshika makalio yake na kuanza kuyatomasa taratibu.

“Ethan sijisikii kufanya jambo lolote nina kuomba uweze kuniacha”

“Mke wangu, nina hamu na wewe”

“Sitaki niache”

Biyanka alizungumza kwa jazba huku akiutoa mkono wangu nao shika makalio yake.

“Kwahiyo hunihitaji uwepo wangu hapa si ndio”

“Vyovyote bwana”

Kauli ya Biyanka ikanifanya nijawe na hasira ya gafla ambayo yote inatoka na uchu wa kimapenzi dhidi yake. Nikamtazama jogoo wangu ambaye tayari alisha simama kwa ajili ya kupata utamu wa Biyanka.

“Mke wangu nina hamu na wewe”

“Sitaki Ethan hunielewi na wewe”

Biyanka alizungumza kwa ukali huku akigeuka na kulala chalia.

“Nahitaji haki yangu”

“Nitolee upuuzi wako. Niache nilale tutakosana Ethan”

“Mimi mpuuzi?”

“Ndio”

Biyanka aliendelea kuzungumza kwa msisitizo. Nikashuka kitandani na kuvaa nguo zangu huku Biyanka akinitazama. Nikachukua funguo ya gari na kuanza kutembea kuelekea mlangoni, msunyo mkali wa Biyanka ukanifanya nisimame na kumgeukia na kumtazama. Nikafungua mlango na kuondoka ndani humu ndani. Nikaelekea eneo lilipo gari langu, nikaingia na kuondoka. Hadi inatimu saa kumi na mbili asubuhi, nikafika ilipo nyumba ya Qeen na Latifa. Kwabahati nzuri nikamkuta Latifa akitoka na gari lake.

“Mkurugenzi vipi mbona asubuhi asubuhi?”

Latifa alizungumza mara baada ya sisi sote kushuka kwenye gari.

“Qeen yupo wapi?”

“Amesha kwenda kazini”

“Mpigie simu muambie nipo hapa nyumbani”

“Kwema lakini?”

“Ndio”

“Ila unaonekana kama haupo sawa Ethan. Hembu niambie ni jambo gani ambalo lina kusumbua”

“Mpigie Qeen”

Latifa akatii kile nilicho muagiza. Akawasiliana na Qeen na kumuomba aweze kurudi nyumbani kwani nina msubiria.

“Karibu ndani nikuandalia kifungua kinywa”

“Nifungulie tu geti, nitaandaa kila kitu mimi mwenyewe”

Latifa akanifungulia geti na nikiangiza gari langu.

“Wewe nenda kazini, muambie sekretari wangu kwamba mafaili yangu yote niyakute mezani kwangu”

“Sawa mkurugenzi, ila ngoja kwanza. Kuna jambo lolote ambalo Qeen amekuudhi?”

“Hajanifanyia jambo la aina yoyote baya ila nina hitaji kumuona tu”

“Sawa mkurugenzi tutaonana ofisini”

Latifa akaingia kwenye gari lake na kuondoka katika eneo hili. Nikaingia ndani na kujilza kwenye hii seble nzuri iliyo pangiliwa vizuri. Japo nimewalipa wasichana hawa kiasi kikubwa cha pesa ila bado wana endelea kufanya kazi katika kampuni yangu. Baada ya kama nusu saa hivi nikasikia mngurumo wa gari, nikakimbilia dirishani na kufungua pazia, nikamuona Qeen akishuka kwenye gari lake, akafunga geti kisha akaanza kutembea kwa mahada kuja ndani humu. Nikajilaza kwenye sofa huku nikijifanya nime lala.

“Hei mambo”

Niliisikisa suti nzuri ya Qeen. Taratibu nikayafumbua macho yangu.

“Umelala jamani, vipi unaumwa Ethan”

Qeen alizungumza huku akiniinamia, kwa haraka nikamvuta karibu yangu na akanilalia kifuani mwangu.

“Ethan”

“Nini”

“Mbona hivyo”

Qeen alilalama kimahaba. Nikamtazama lispi zake zilzo nona vizuri, taratibu nikaanza kuzinyonya huku nikianza kuyaminya makalio yake kwa nguvu na kuzidi kuamsha hisia zangu za mapenzi.

“Ethan jamani una nini leo”

Qeen alizungumza huku akinitazama kwa macho yaliyo mlegea.

“Nahitaji unifanyie jambo”

“Jambo gani Ethan”

“Nataka unibebe ujauzito wangu na unizalia mtoto sawa”

Qeen macho yakamtoka, akajawa na mshangao mkubwa sana huku nikianza kuyasikia mapigo yake ya moyo yakianza kumuenda kasi huku jasho likianza kumtiririka usoni mwake ingali ndani ya seble hii kuna hewa kali ya A/C.


Qeen kwa haraka akaniachia na kusimama huku akishika kichwa chake huku akionekana kama mtu aliye changanyikiwa kiasi.

“Qeen vipi?”

Nilizunguza huku nikikaa kitako na kumtazama usoni mwake. Qeen hakunijibu kitu chochote zaidi ya kuendelea kuonekana akiwa amejawa na wasiwasi mwingi sana usoni mwake.

“Niambie una tatizo gan?”

“Ethan ulisha nitamkia kwamba mimi hunipendi. Una mwanamke wa maisha yako ambaye utakwenda kuzaa naye siku si nyingi. Sasa unataka uzae na mimi ili iweje?”

Qeen alizungumza kwa msisitozo huku akiendelea kuhema mithili ya mtu aliye kimbia mbio ndefu.

“Qeen hembu tambua kwamba, nina hitaji mtoto kutoka kwako. Nipo tayari kumlea mtoto huyo kwa garama yoyote”

“Hapana Ethan wewe una nitamani. Hunipendi kabisa, moyo wako haupo kwangu, moyo wako haunifikirii mimi. Umenifanya mimi kama kibaraka wa kutimiza haja zako. Mimi na Latifa tumesha wahi kushiriki kitanda kimoja ili kukuridhisha wewe, unahisi hayo ni mapenzi au uchangudoa”

Qeen alizungumza huku machozi yakiendelea kumwagika usoni mwake. Haya anayo yazungumza hakika yakaanza kunifanya nihisi kujutia sana moyoni mwangu.

“Ethan kuna mambo mengi nilsha jikatia tamaa kwako. Kuna mambo mengi ambayo kwako natambua kwamba hayato wezekana. Mimi ni mfanyakazi wako tu na nitaendelea kubaki kuwa mfanyakazi wako. Sitaki siku Biyanka aje kuniangamiza, kwanza ni bosi wangu, pili ana pesa kulilo mimi na tatu anajuana na watu wengi serikalini kuliko mimi, je unataka nitekwe kama wanavyo tekwa tekwa watu eheeee?”

Qeen aliendelea kuzungumza huku sasa hivi akiangua kilio. Taratibu nikasimama na kumsogelea nikajaribu kumshika kiono chake, ila akautoa mkono wangu kwa nguvu.

“Qeen tambu mimi ni binadamu”

“Ndio hata mimi ni binadamu. Ulipo nikana tena ukamuambia kabisa na Latifa akaja kunikoromea ulihisi moyo wangu ni wa chumba, ulihisi moyo wangu hauto umia si ndio. Ethan nilikonda kwa ajili yako, niliumia kwa ajili yako, nilikuwa silali kwa ajili yako. Hadi kichwa changu kikawa kinafikiria kufanya mambo mabaya dhidi yako ila nikashindwa kufanya hivyo, unahisi kidonda kile kitapona kirahisi”

“Mambo mabaya!!?”

“Ndio mambo mabaya. Ethan mimi ni mwanamke ambaye nikipenda huwa nina penda, sinaga swala la kupenda robo robo na wala simpendei mwanaume utajiri wake, simpendei mwanaume uzuri wake. Ila vitu nilivyo kuwa nina vitaka wewe Ethan kwako siwezi kuvipata”

Qeen aliendelea kulia kwa uchungu sana hadi machozi na mimi yakaanza kunilenga lenga.

“Ethan wanawake tuna hitaji, heshima, muda wa mwanaume, tunahitaji kujaliwa ila wewe kwako siwezi kupata. Acha niendelee kuishi maisha ya kusagana na Latifa kwa maana kila ninapo hitaji kukata kiu yangu yeye ananipa kile ninacho kitaka”

Sikustuka sana kusikia swala la yeye na Latifa kusagana.

“Qeen sawa natambua kwamba nime kukatili kwa kiasi kikubwa, ila tambua kwamba nina kuhitaji”

“Ethan mimi sio mnafki, kusema kweli sikuhitaji”

“Eheee?”

“Ndio sikutaki na ninaomba nirudi kazini. Utabaki kuwa mkurugenzi wangu hadi pale utakapo amua kunifukuza kazi”

Qeen mara baada ya kumaliza kuzungumza hivyo akachukua pochi yake mezani na kuanza kutembea kwa kasi kuelekea mlangoni. Nikamuwahi mlangoni kwa haraka na kumzuia.

“Nina kuomba nipite mkurugenzi”

“Siwezi kukuacha upite”

“Nahitaji kupita tafadhali, nakuomba uweze kuniacha”

“Mbona unabadiliak badilka wewe mwanamke. Ulipo kuja si nilikunyonya denda pale, sasa hichi unacho kifanya hapa ni nini. Unataka kunionyesha kwamba wewe ni jauri au?”

“Mkurugenzi nina hitaji kwenda kazini, nafasi yangu sijamuachia mtu anishikie. Tafadhali nina kuomba mkurugenzi”

“Hakuna kutoka”

“Tafadhali”

“NIMEKUAMBIA HAKUNA KWENDA POPOTE”

Nilizungumza kwa ukali sana hadi Qeen akatetemeka. Macho yangu yaliyo jawa na hasira, yakaanza kumfanya Qeen aanze kurudi rudi nyuma taratibu hadi akaa kwenye moja ya sofa huku akiendelea kunitazama kwa woga.

“Unahisi kwamba sijaona wanawake wa kuzaa nao EHEEE!!?”

“Ninahitaji kuzaa na wewe kwa maana nina hitaji mwanangu aishi maisha mazuri. Umri wangu unazidi kwenda, nahitaji kuwa baba sasa”

“Ethan sitaki mwanaume ambaye nitazaa naye aje kumtesa mwanangu. Sitaki mwanaume ambaye nitazaa naye anitese mbeleni, sitaki Ethan”

“Nalitambua hilo nakuahidi sinto kutesa na utaishi kwa amani sana katika maisha yako”

Qeen akanitazama kwa macho makali huku akiendelea kububujikwa na machozi.

“Unahitaji kuzaa na mimi kweli?”

“Ndio”

“Basi ninakupa masharti matatu kama hoto yakubali basi hoto kuja kukaa na kupata mtoto kwangu”

“Masharti matatu?”

“Ndio”

“Ehee ni yapi hayo?”

“Nahitaji tukapime kila kitu kwenye miili yetu, kuanzia HIV, na vipimo vyote ili hata tukizaa nina imani kwamba mwanangu atakuwa amezaliwa katika ile hali ya afya ambayo nina ihitaji”

“Sharti la pili?”

“Utalifahamu mara baada ya kumaliza sharti la kwanza”

“Kwa nini?”

“Si unahitaji kuza na mimi, kama unakubaliana na hilo. Niambie hata sasa hivi tukakutane na daktari na kupima kila kitu”

Nikashusha pumzi taratibu huku nikimtazama Qeen usoni mwake.

“Sawa nipo tayari”

“Kweli Ethan?”

“Ndio nipo tayari laiti kama ningekuwa sipo tayari mimi nisinge weza kukubaliana na wewe katika hilo”

“Sawa tutumie gari langu au lako kwenda hospitali?”

“Lako sihitaji gari yangu iweze kuonekana huko mitaani. Ila naomba nitafutie kofia ili nikivaa nisiweze kuonakana. Tambua kwamba mimi ni mtu maarufu sana”

“Sawa hili halina tabu, au kuna jengine?”

“Hakuna ni hilo”

Qeen akanyanyuka na kuingia chumbani kwake, baada ya muda akarudi akiwa ameshika kofia nyeusi inayo fanania na tisheti hii nyeusi niliyo ivaa.Nikavaa kofia kisha tukatoka ndani humu. Safari ya kueleka hospitalini ikaanza huku tukikubaliana ni hospitali gani tunatakwa kwenda kufanya vipimo. Mawazo juu ya maamuzi yangu ninayo yafanya kwa Qeen yakaanza kunitawala.

‘Kwa nini nisimuombe Camila anizalie, ikiwa mimi na yeye tumetokea mbali sana toka utotoni?’

‘Ila Camila kwa sasa sidhani kama ana weza kukubali kuzaa na mimi ikiwa kuna kazi amesha anza kuifanya’

‘Ehee Mungu nisaidie’

“Mbona una mawazo sana?”

Qeen alizungumza huku akisimamisha gari taratibu. Nikatazama magari mengi yaliyo simama katika hospitali hii ya Agakan.

“Hakuna”

“Tumesha fika hospitali, twende ndani”

Nikashusha pumzi taratibu kisha tukashuka kwenye gari. Tukaingia ndani na Qeen akazungumza na muhudumu aliyopo mapokezi. Tukaandikisha majina yetu kisha tukaelekezwa ni eneo gani tuelekee. Tukafika kwenye ofisi ya daktari tuliye elekezwa, na kuwakuta watu wanne ambao kila mmoja ana onekana yupo na mpenzi wake. Tukasalimiana nao kisha tukaa kwenye foleni hii.

“Qeen una uhakika na hili ambalo tunalifanya?”

Nilimuuliza Qeen kwa sauti ya chini chini.

“Ndio nina uhakika huo ndio maana nilizungumza.”

Mlango wa chumba hichi cha daktari ukafunguliwa na akatoka jamaa mmoja na mke wake huku mwanamke huyo akionekana kububujiwa na machozi usoni mwake.

“Nilipo kua nina kukanya kila siku uachane na vijitoto vya mtaani ukawa una niona mimi mjinga. Ohoo unaona mimi malaya nje, haya mwanzako nilikuwa ninatumia kinga, wewe ukaenda kujineng’enesha huko uepewa Ukimywa, utakufa mwenzio huo ushauri nasaa huko ndani mimi hata sitaki kuusikia. Umenielewa”

Mwanaume huyo alizungumza kwa ukali sana huku akimtazama mke wake huyu anaye endelea kulia kwa uchungu. Mapigo ya ya moyo yakazidi kunienda kasi sana, nikaanza kukumbuka mapenzi niliyo yafanya kuanzi kwa Camila, Biyanka kisha Qeen na Latifa.

“Ila baba Light…”

“Wewe mwanamke mimi sio mume wako. Twende ukachukue kilicho chako urudi kwenu ukajiuguze vizuri ukimwi wako. Unahisi nitataka kufa mimi kijinga nyooo”

Mwanaume huyu alizungumza huku akimshika mkono mke wake na wakaondoka huku wakikokotana. Watu wote hapa tukabaki katika hali ya sinto fahamu. Watu ambao ni zamu yao kuingia ndani ya chumba hichi cha daktari kwa ajili ya ushauri nasaa kisha wapime wakasita kunyanyuka mara baada ya kusikia majina yao kuitwa na daktari.

“Munaweza kutangulia?”

Jamaa huyo aliwaambia hawa watu tulio kaa nao karibu.

“Hapan ni zamu yenu kwenda”

“Mmmmm”

Daktari wa kiarabu akatoka ndani ya chumba chao.

“Janet na John wapo jamani?”

Daktari huyu aliuliza huku akitutazama kwenye nyuso zetu.

“Tupo”

Walijibu kiunyonge. Wakanyanyuka na kuingia ndani ya chumba hicho cha daktari. Nikaitazama mikono ya Qeen na kuiona jinsi inavyo mtetemeka kwa woga, ujasiri wote ambao alikuwa akinionyesha nyumbani wote umeyanyuaka mithili ya barafu juani. Nikamshika mkono wake wa kulia na kumtazama usoni mwake.

“Una jiamini katika hili?”

Nilimuuliza Qeen kwa sauti ya chini sana.

“Ehee?”

“Upo tayari kwa ajili ya kupima?”

“Ehee ndio”

Qeen alijibu huku akishusha pumzi nyingi sana. Wawili hao walio ingia wakatoka ndani kwa daktari huku wakiwa na furaha sana. Wakafwata hawa wengine na tukabakia sisi wawili. Simu yangu ikaita, nikaitoa mfukoni na kukuta ni namba ya Biyanka. Qeen akanitazama usoni kwa sekunde kadhaa, nikaipokea na kuiweka sikioni.

“Ndio”

“Upo wapi mume wangu”

Nikamtazama Qeen kwa jicho la kuiba kisha nikasimama na kusogea pembeni kidogo.

“Endelea kulala kuna mambo nina yashuhulikia”

“Mambo gani jamani mume wangu”

“Mambo muhimu nitakuambia badae”

Nikakata simu na kuizima kabisa. Nikarudi sehemu alipo kaa Qeen akanitazama kwa macho makali ambayo kwa kuyatafsiri kwa haraka haraka ni kwamba yamejaa wivu ndani yake. Wawili hawa wakatoka huku nyuso zao zikiwa katika hali ya kawaida tu. Tukaitwa majina yetu na kuingia ndani ya ofisi hii. Ofisi hii imegawanyika katika maeneo mawili, moja wapo likiwa ni la kukaa daktari huku jengine likwa ni eneo la vipimo.

“Karibu sana wapendwa”

Daktari alizungumza kwa upole na unyenyekevu mkubwa sana.

“Shukrani”

“Ahaa labda niwaulize swali dogo tu. Mupo kwenye mahusiano kwa kipindi gani?”

“Sisi?”

Qeen alizungumza huku akionekana dhairi kwamba hajiamini kabisa.

“Ndio”

“Sio muda mrefu, ni wiki mbili”

Niliwahi kumjibu daktari huku nikimtazama usoni mwake.

“Ohoo sawa sawa. Je mumedhamiria kabisa kuja kutazama afya zetu?”

“Ndio maana tupo hapa daktari”

Niliendelea kujibu kwa ujasiri huku nikimkazia macho Qeen ambaye ujanja wote umemuishia. Daktari akaanza kutupa ushauri sanaa. Ushari ambao hakika unatia matumaini makubwa sana. Ikafika muda wa kupima, halikuwa jambo gumu sana kwani kati yetu hakuna anaye ogopa kuchomwa kisindano kidogo.

“Baada ya dakika kadhaa majibu yenu yatakuwa tayari hivyo kuweni na amani tu”

Simu ya Qeen ikaita, akafungua mkoba wake, akaitazama kwa muda akataka kutoka nje ili aweze kuipokea, ila nikawahi kumshika mkono na kumkalisha chini.

“Kata simu, utazungumza naye baadaye’

“Baby ni simu muhimu?”

“Kutoka kwa nani?”

“Eheee?”

“Kutoka kwa nani ikiwa mimi ndio mkurugenzi wako. Tusubirie majibu mama”

Nilizungumza kwa msisitizo na kumfanya Qeen azidi kutetemeka kwa woga hata kukata simu yanyewe akashindwa na kujikuta akiirudisha ndani ya pochi yake bila kufanya jambo lolote lile.



Ukimya ukaendelea kutawala ndani ya hichi chumba. Kila muda macho yangu yanamtazama Qeen usoni mwake, daktari akanyanyuka na kuingia katika kijichumba chake cha vipimo. Baada ya dakika kama tano hivi akatoka akiwa na karatasi mbili mkononi mwake. Akakaa kwenye kiti chake huku uso wake ukwia umejawa na tabasamu pana sana.

“Ahaa majibu yenu yapo tayari”

Dokta alizungumza huku akijiweka vizuri kwenye kiti chake.

“Labda nianze kutoa majibu ya nini?”

“Yangu”

Nilahi kuzungumza.

“Sawa, bwana Ethan, majibu yako yanaonyesha kwamba upo salama. Damu yako haina maambukizi ya aina yoyote ya virusi vya Ukimwi”

Nikashusha pumzi kubwa sana huku nikimtazama daktari kwa furaha sana. Nikamtazama Qeen na kumuona akiwa amefumba macho yake mithili ya mwanafunzi wa kike anaye subiria kuchapwa fimbo mkononi mwake.

“Bi Qeen majibu yako yanaonyesha kwamba……”

Qeen akanyoosha mkono wa kulia kumzuia daktari kuzungumza kile alicho panga kukiongea na kutufanya mimi na dokta kumshangaa sana.

“Dokta basi wewe mpatie Ethan majibu yake. Am out”

Qeen alizungumza kwa upole huku akinyanyuka kwenye kiti chake. Nikamkalisha huku nikimshika mkono wake.

“Dokta endelea”

“Naye pia majibu yake yanaonyesha kwamba hana maambukizi yoyote ya virusi vya ukimwi”

“Dokta acha utani?”

Qeen alizungumza huku akijaribu kutabasamu na yeye.

“Am professional dokter na nina uhakika na kazi yangu. Na nina uhakika kwamba hauna maambukizi ya ugonjwa huo. Ila kupima kwa sasa isiwe mwisho wa kupima. Inabidi mara baada ya miezi mitatu tena muweze kurudi kisha mupime tena”

“Ahaa hii inatosha dokta”

Qeen alizungumza huku akijawa na furaha kubwa sana hadi daktari akatabasamu.

“Haitoshi, ni vyema muwe na utaratibu wa kucheki afya zenu mara kwa mara ili muzidi kujiamini sana katika mahusiano yenu”

“Tunashukuru sana daktari. Mimi nitahakikisha mara baada ya miezi mitatu tutarudi hapa na huyu bibie”

“Wewe”

“Hakuna cha wewe, hapa tutarudi tena na tena”

“Karibuni sana, tuzidi kumuomba Mungu awabariki ili siku mukirudi basi munikute mimi tu”

“Sawa daktari. Ahaa tunahitaji kupima maswala ya uzazi kwa maana kwa sasa tunahitaji kutafuta mtoto, je ni ofisi gani ambayo munatoa huduma hiyo hapa hospitalini kwenu”

“Ohoo hayo ni maamuzi mazuri sana. Watu wengi huwa wanajikuta wanazaa pasipo kupima kujua kama ni nani kati yao anaweza kuwa na matatizo ambayo kwa namna moja mama au baba anaweza kumrithisha mtoto wake”

“Ni kweli dokta ndio maana tumeamua kuja kupima”

“Basi ngoja niwandikie barua muende kwa daktari huyu ili iwe rahisi kwa nyinyi kupata huduma”

“Sawa”

Daktari huyu akatuandikia barua kisha tukatoka ofisini kwake na kuelekea katika ofisi ya dakatri huyo. Tukapima vipimo vyetu vya uzazi na kuombwa tuweze kusubiria vipimo. Furaha kubwa ikaendelea kutawala kati yetu huku kila mmoja akioneka kuwa na shauku ya kupata mtoto. Muda wa majibu ukafika na tukaitwa ofisi kwa daktari huyo.

“Karibuni tena”

Daktari huyu alizungumza.

“Tunashukuru”

“Majibu yenu ni mazuri kiasi japo sio sana”

Tukatazamana na Qeen huku furaha ambayo tulikuwa nayo taratibu ikianza kupungua.

“Vipimo kwa baba hapa inaonyesha kwamba mfumo wako wa uzazi upo salama kabisa na hauna matatizo. Ila tukirudi kwa mama hapa, inaonyesha kwamba una tatizo la Ugumba”

Qeen akastuka sana huku nikimshuhudia akianza kutetemeka mikono yake. Hata nami moyoni mwangu nikajikuta nikipoteza furaha kwani hili hatukuritarajia kabisa.

“Ila usiogope. Ugumba sio ungonjwa ambao utakufanya wewe ushindwe kato pata mtoto. Ila lazima uweze kukubalina na jinsi ya kupambana na tatizo hilo”

“Dokta wewe niambie dawa ya aina yoyote na kwa garama ya aina yoyote nipo tayari kumnunulia mpenzi wangu”

Daktari akatabasamu kidogo huku akinitazama.

“Unajuwa watu wengi wanapo sikia tatizo la ugumba kwa haraka haraka wanahisi kwamba labda lina maambukizi au halitibiki. Nikirudi kwenye kauli yangu ya awali nilipo sema kwamba majibu ni mazuri ila si sana, nilikuwa nina maanisha kwamba, tatizo lako bibie halijafika mbali sana. Halijafika kwenye hatua ya kuto kutibika, ila ndio kwanza linaanza. Hivyo inabidi uweze kupambana na vyanzo au chanzo kinacho sababisha tatizo hilo na endapo utafanikiwa kabisa kuachana na hilo jambo basi unaweza kupona na kupata mtoto kama wanavyo pata watu wengine”

“Moja unatakiwa kuacha kunywa pombe kali kabisa. Pili unatakiwa kuepukana sana na msongamano wa mawazo na endapo utafanikiwa kufanya hayo mambo mawili, baada ya miezi mitatu rudini tena kwa vipimo zaidi?”

“Hakuna dawa yoyote dokta zaidi ya hayo maelezo?”

“Ndio kijana, hakikisha kwamba una msimamia mkeo ana pambana na hali hiyo hadi ana rudi katika hali yake ya kawaida”

“Sawa dokta nita hakikisha kwamba nina fanya hivyo na nina shukuru sana”

“Sawa”

Tukatoka chumbani hapa kwa daktari, tukarudi mapokezi na kufanya malipo yote ya vipimo ambavyo tumetumia ndani ya hospitali hii kisha tukaondoka huku nikiendesha gari. Njia nzima Qeen ana tiririkwa na machozi kiasi cha kumfanya apoteze furaha kabisa.

“Sasa unavyo zidi kuendelea kulia hivyo ndivyo jinsi unavyo jipa mawazo”

“Ethan unahisi kweli nitapona mimi?”

“Ndio, si daktari umemsikia, kwamba acha kunywa mapombe makali. Yale mapombe muliyo yajaza mule ndani kwenu si ufahari kuendelea kuyatumia. Umenielewa”

“Ethan sikutegemea kukutana na mambo kama haya”

“Si wewe tu hata mimi, ila jambo la msingi ni kuhakikisha kwamba unafwata yale yote ambayo dokta amekushauri umenielewa?”

“Sidhani kama nitaweza?”

“Hee udhani kama huta weza ikiwa tatizo ni lako?”

“Nimesha zoea kunywa sana kutokana na mawazo yangu binafsi”

“Sasa ndio uache hayo mambo sawa”

“Mmmm”

“Wewe sema mmmm tu”

Tukafika nyumbani, Qeen akapitiliza moja kwa moja hadi chumbani kwake. Nikaingia na kumkuta akiwa amelala kitandani huku akilia kwa uchungu sana.

“Kuendelea kukia hivyo ndio kutakufanya uzidi kujawa na msongamano wa mawazo Qeen”

“Ethan wewe hujui ni jinsi gani nilivyo umia”

“Natambua ila kutokana dokta mwenyewe amesema kwamba ina wezekana wewe kupona hilo tatizo hakuna haja ya kuendelea kulia lia wala kuwazia. Kikubwa ni wewe kupambana na hii hali”

“Naomba nilale, labda nikiamka nitakuwa sawa”

“Ehee?”

“Naomba nilale”

Nikamtazama Qeen kwa sekunde kadhaa kisha nikanyanyuka na kutoka ndani hapa. Nikapanda kwenye gari langu na kuondoka nyumbani hapa. Moja kwa moja nikaelekea ofisini kwa mwana sheria wangu mkuu na kwa bahati nzuri nikamkuta.

“Mkurugenzi vipi mbona hata taarifa?”

“Wee acha yaani kwa mawazo haya nina weza kuchanganyikiwa na kunikuta nimejiingiza mtaroni humo na gari langu”

“Ohoo kuna nini tena?”

“Nahitaji msaada wako”

“Msaada gani”

“Nataka kupata nyumba nzuri yenye hadhi nzuri hapa jijini Dar, sasa sijajua utanisaidiaje?”

“Nyumba ya kupanga au kununua?”

“Kununua kabisa, kwa mana zitakuwa ni baadhi ya asset zangu ninazo endelea kuwekeza jijini hapa”

“Ahaa..sawa. Nipe siku hii ya leo niweze kuulizia kwa madalali maarufu hapa mjini kisha nitakufahamisha bosi wangu”

“Nashukuru, naomba iwe eneo zuri na salama. Nina imani kwamba una nifahamu sipendi yale mambo ya uswahilini uswahili”

“Natambua hilo mkuu”

“Sawa, acha mimi niondoke hapa kwa maana nina mizunguko kadhaa”

“Sawa”

Nikarudi lilipo gari langu. Kabla sijaliwasha nikamuona Ethan akiwa amekaa katika siti ya nyuma huku akinitazama.

“Vipi?”

“Leo ulitaka kufanya vituko vya karne”

“Kwa nini?”

“Hivi unahisi kweli ningeruhusu uzae na kale kademu?”

“Qeen?”

“Unajua nani nina mzungumzia?”

“Kwani ana kasoro gani?”

“Acha kufanya maamuzi ya ajabu ikiwa bado sihitaji kwa sasa wewe uweze kupata watoto”

“Kwa nini?”

“Unahisi kwa sasa una muda wa kutazama mtoto na kulipiza kisasi. Kumbuka ndio kwanza vita yako inaanza, yale uliyo yafanya kwa mzee Poul Mkumbo usihidi kwama ni ushindi bado una takiwa kujipanga zaidi. Umenielewa”

“Unajua Ethan muda mwengine ni kweli unanisaidia sana. Ila tambua kwamba hata mimi nina akili na maamuzi yangu ya kuweza kufanya katika kila jambo. Tafadhali muda mwengine unatakiwa kunipa muda wa kufanya kile kitu ambacho mimi nina kihitaji”

“Mmmm hivyo?”

“Ndo hivyo nina hitaji kuwa na maamuzi, nina hitaji kuwa mtu ambaye nina weza kupanga mambo yako”

“Sawa nimekuelewa. Tutaonana”

Ethan akapotea katika eneo hili. Nikawasha gari na kurudi ofisini kwangu, nikaiwasha simu yangu na meseji mfululizo za Biyanka zikaanza kuingizana. Meseji zote hizo zimejaa malalamiko huko akiniomba msamaha kwa kitendo alicho nifanyia asubuhi. Kabla hata sijamaliza kusoma meseji zake, simu yangu ikaanza kuita na kuitazama namba ya Biyanka kisha taratibu nikaipokea na kuiweka sikioni mwangu.

“Ethan mume wangu natambua kwamba nimekufanyia makosa jamani. Nakuomba uweze kunisamehe”

“Mbona nimekusamehe”

“Hapana umezima simu siku nzima jamani. Natambua kwamba unajua ni kitu gani ambacho kinaendelea kwenye hii familia yangu, nakuomba usinikatili kwa kiasi hicho”

“Sawa nimekuelewa”

“Ethan mume wangu mbona una nijibu kimkato mkato hivyo”

“Tafadhali nipo ofisini nina kuomba niweze kufanya kazi. Sasa ni muda wa kuhakikisha kwamba biashara zangu zinazidi kusonga mbele. Tafahali nina kuomba uweze unipa muda wa kufanya kazi yangu”

Nikakata simu huku nikiwa nimejawa na jazba kidogo. Sekretari wangu akaingia huku akiwa na mafaili kadhaa mkononi mwake.

“Hayo yana nini?”

“Ni baadhi ya mikataba ya matanagazo ambayo kampuni imengia na baadhi ya wasanii pamoja na timu za mpira kama vile ulivyo agiza hivyo unatakiwa kuidhinisha tu mikataba iweze kupitishwa na kazi rasmi tuweza kufanya na wa wahusika”

Nikampa ishara sekretari wangu ayaweke mafaili hayo juu ya meza yangu. Akatembea kwa hatua kadhaa hadi mlangoni kisha akageuka na kunifwata hapa nilipo.

“Mkurugenzi, madam Biyanka alinipigia simu na kuniulizia kama upo ofisini ila nikamueleza kwamba haujafika bado na nilijaribu kukupigia na simu yako sikuipata hewani”

“Ohoo nitalifanyia kazi hilo jambo”

“Sawa”

Sekretari akatoka ndani humu, nikachukua faili moja na kujaribu kulipitia ila kutokana na msongamano wa mawazo ulio nitawala nikajikuta nikishindwa kabisa kufanya chochote. Nikanyanyuka kwenye kiti niliacho kikalia na kutoka ndani humu. Nikaingia kwenye lifti na moja kwa moja nikashuka hadi kwenye eneo la maegesho ya magari yaliyopo eneo la chini kabisa la gorofa hili. Nikaingia kwenye gari langu n ataratibu nikaanza kutoka humu ndani. Nikafika getina na walinzi wakanifungulia geti langu, kitendo cha kutokeza tu barabarani, gafla gari aina ya Land Cruser ikasimama mbele yangu na kunilazimu kufunga breki za gafla. Vioo vikashushwa na wakajitokeza watu wawili walio funika nyuso zao huku mikononi wakiwa wameshikwa bunduki aina ya mashine gun na wakaanza kunishambulia kwa kunimiminia risasi nyingi sana katika gari langu hili.



Uzuri wa gari langu ni gumu sana katika kuingiza risasi na hata risasi zote wanazo nishambulia kwa bahati nzuri zinaishia kupiga kwenye kioo. Walinzi wangu kwa haraka nao wakaanz akujibu mashambulizi ya wavamizi hawa huku nikijitahidi kurudisha gari yangu nyuma na kurudi eneo la kampuni. Gari la wavamizi likaondoka kwa kasi eneo hili. Hali ilipo anza kuwa shwari, walinzi wangu wakaniomba nishuke kwenye gari, na taratibu nikafungua mlango wa gari langu huku nikiwa na wasiwasi mwingi sana. Wakaanza kunizunguka na kuingia ndani ya ofisi za kampuni yangu ambapo napo tukakuta hali ya kutaharuki kwa wafanyakazi. Wakaniingiza kwenye lifti na kwa pamoja tukaekea hadi ofisini kwangu. Nikaingia na mkuu wao wa ulinzi huku walinzi wengine wakibaki mlangoni kuimarisha ulinzi.

“Nina imani kwamba hapa utakuwa salama mkuu”

Mkuu huyu wa kikosi hichi cha ulinzi nilicho kiajiri hapa kwenye kampuni yangu alizungumza huku akichungulia chungulia kwenye nje ya gorofa langu. Akaanza kufunga mapazia ya ofisi zangu kisha akawasha taa za ndani ya ofisi hiii.

“Mkurugenzi”

“Mmmm”

“Upo salama?”

“Ehee!!?”

“Ngoja nikuchukulie maji ya kunywa”

Alizungumza kisha akatoka ndani humu. Ukimya huu wa hapa ufisini kwangu kunanifanya niweze kuyasikia vizuri mapigo yangu ya moyo jinsi yanavyo dunda kwa nguvu. Kwenye maisha yangu nimefanya mambo ya ajabu ajabu mengi, ila kwa hili la watu kunivamia kwa lengo la kutaka kuniangamiza hakika sijawahi kulishuhudia kabisa. Akaingia mkuu wa walinzi wangu huku akiwa ameshika chupa ya maji, akaifungua na kuniwekea mezani.

“Kunya kidogo uweze kuituliza hiyo hali ya presha inao kutawala”

Nikayatazama maji haya kisha taratibu nikaanza kuyanywa, ila kwa woga ambao bado ninao hakika sikuweza kuyafikisha haya maji hata nusu chupa. Mlango ukafunguliwa na akaingia mlinzi mwengine.

“Mkuu askari na waandishi wa habari wamefika eneo hili”

“Waruhusu askari wandishi wa habari wasiingie ndani ya geti sawa”

“Sawa mkuu”

Akaondoka eneo hil. Nikashusha pumzi nyingi huku nikijitahidi kuirudisha akili yangu katika hali ya kawaida.

“Mkurugenzi unahisi ni kina nani ambao wamekuvamia?”

“Unasema?”

“Unahisi ni kina nani ambao wamekusudia kukuvamia na kukunamaliza?”

“Yaani wala sifahamu aisee, hakuna mtu aliye kufa kweli?”

“Hapana vijana wangu wote wapo salama na wameifanya kazi yao kikamilifu kama vile jinsi ulivyo tuamini kutupa kazi ya kukulindia kampuni yako”

“Ohoo Mungu wangu. Au kuna mtu watakuwa wanamtafuta?”

“Sijajua mkurugenzi labda hilo swali nilirudishe kwako kwa maana gari yako kwa mara kadhaa amekuwa akiitumia mke wako na ukitegemea kwamba mke wako baba yake alikuwa ni mwana siasa, sasa huwenda kuna watu wana hitaji kulpa kisasa dhidi ya familia ya mkweo ndio maana wakakushambulia wewe”

“Gari yangu imepona?”

“Siwezi kusema ndio au hapa na kwa maana sijalichunguza kabisa gari lako.”

Akaingia mkuu wa polisi wa kanda maalumu hapa Dar es Salaam. Si mara yangu ya kwanza kukutana na huyu mzee, kwani nilisha wah kushirikiana naye katika siku za juma juu ya kuokoa maisha ya mtoto Clara amabaye hadi sasa hivi bado yupo chini ya uangalizi wangu.

“Ethan vipi tena?”

“Yanai hata sielewi mzee wangu karibu ukae”

Mkuu wa polisi kanda maalumu akaka kwenye kiti changu huku akinitazama usoni mwangu.

“Macho yako bado yana presha inabidhi uweze kupata muda ili ukitulia kidogo tuweze kuhojiana”

“Sawa”

“Umewasiliana na familia?”

“Hapana”

“Ngoja nimpigie mke wako kwanza”

Mkuu huyu wa polisi alizungumza huku akitoa simu yake mfukoni na kuanza kuwasiliana na Biyanka akamtaarifu juu ya tatizo lililo nisibu. Baada ya kumaliza kuzungumza na Biyanka akaka kata simu.

“Bibie amesema kwamba yupo Bagamoyo ila atafika hapa haraka awezavyo”

“Sawa”

“Vijana wangu wanaendelea kufanya mahojiano yao na vijana wako. Tunahitaji kuhakikisha msako mkali unafanyika ndani ya jiji la Dar es Salaam”

“Sawa”

Simu yangu ikaita na nikaitoa mfukoni na kukuta ni Biyanka ndio anaye nipigia. Nikaitazama kwa sekunde kadhaa huku nikijishauri ni nipokee ama nisipokee, ila mwishowe nikajikuta nikipokea.

“Mmmm”

“Mume wangu jamani upo salama”

Biyanka alizungumza kwa sauti iliyo jawa na wasiwasi mwingi sana.

“Ndio nipo salama”

“Ohoo najiandaa nina kuja sasa hivi na usiondoke hapo ofisini, sawa baba yangu”

“Sawa”

“Ohoo Mungu wangu, ni nini hichi”

Nikakata simu, hata kabla dakika moja haijaisha simu yangu ikaanza kuita tena na kukuta ni namba ya mama mkwe. Nikaipokea taratibu.

“Mama”

“Ethan mwanangu, ohoo nashukuru kwa kuisikia sauti yako tena. Vipi umejeruhiwa?”

“Hapana mama yangu”

“Yaani huyo kama si baba yako aliye tuma hao vijana sijui. Ila nafsi yangu na moyo wangu vyote vina hisi ni yeye aliye fanya huo upuuzi wake”

Nikastuka kidogo kwa kusikia kauli hii ya mama mkwe.

“Kwa nini mama unazungumza hivyo?”

“Huyo ni mshenzi. Hafai kabisa ni shetani, yaanii huyo mzee hanaga fadhlila kabisa. Huwa ana jifikiriaga yeye kama yeye. Yupo tayari kua hata ndugu zake na alisha wahi kufanya hivyo, sasa sembuse wewe mkwe wake hapana hawezi kushindwa. Kuwa naye makini sana mwanangu, ndio maana uliona nina hakikisha kwamba nina kutetea kwani alitaka kukuingizakwenye mabiashara yake ya ajabu ikiwa akili yako ni smart sana na haihitaji wewe kujiunga kwenye hayo mambo mwanangu”

Mama mkwe alizungumza kwa msisitizo na kuifanya akili yangu kwa sasa kuanza kufunguka taartibu. Vita ya kimya kimya mbayo ninaifanya kwa mzee Poul Mkumbo, yeye mwenzangu ameamua kuirudisha mubashara.

‘Ila atakuwa amejuwaje, hapana?’

Niljiuliza huku nikikosa jibu sahihi kwa maana kazi zote ninazo zifanya kwa mzee Poul Mkumbo ninatumia ukimya ua usiri wa hali ya juu.

“Umenielewa baba yangu”

“Ndio mama”

“Huyo baba yako kaa naye mbali. Kwenye hiyo familia mtu anaye mpenda pekee ni Biyanka tu ila wewe atakuwa tayari kukuondoka duniani. Isitoshe mwanangu una zifahamu siri zake, hembu kuwa makini naye umenielewa”

“Nimekuelewa mama”

“Sidhani kama hapa Tanzania una maadui wakubwa sana hadi wa kutaka kukuaa mchana kweupe kiasi hicho sidhani. Ila kama kweli huyu basi nina asilimia mia moja atakuwa ni Mkumbo.”

“Ila mama unahisi kwamba…..”

Nikajikuta nikikatisha swali langu mara baada ya kumtazama mkuu huyu wa polisi wa kanda maalumu. Mzee huyu ni kibaraka mkubwa sana wa mzee Poul Mkumbo. Nikalikatisha swali langu.

“Tutaongea baadae”

“Sawa mwanangu. Ila nimedumu na mkumbo huu sasa ni mwake wa thelathini na tano, hivyo naelewa ubaya wake wote. Hivyo naomba kukusisitizia kwamba kuwa makini sana mwanangu”

“Sawa mama nashukuru na nimekuelewa”

“Haya baadae”

Mama mkwe akakata simu na taratibu nikashusha pumzi yangu kwani sikuweza kumfikiria mzee Mkumbo kwa haraka haraka kiasi hichi ila kwa haya aliyo niambia mama mkwe ni lazima niweze kumshuku mzee Mkumbo kwa asilimia zote kwamba yeye ndio aliye hitaji kuniua.

“Vipi mama ana semaje?”

“Ana nipa pole?”

“Hilo tu?”

“Mambo mengine ni yangu na mama yangu na sinto hitaji mtu mwengine aweze kufahamu. Wasimamie vijana wako kufanya kazi yao ofisini kwangu na wakimaliza nina omba waondoke”

Nilizungumza kwa msisitizo huku nikimtazama mkuu huyu wa polisi kanda maalumu hapa Dar es Salaam.

“Ethan ila kumbuka kazi yangu ni kulinda raisi, hivyo nina paswa kukulinda na wewe”

“Nina vijana wangu wana tosha katika kulinda ulinzi wangu kama walivyo fanya pale getini. Asante sana mkuu nakuomba uweze kunipa nafasi hapa ofisini kwangu”

Mkuu huyu wa polisi akanitazama kisha akanyanyuka huku akionekana kuto ridhika kabisa na hili nililo mueleza. Akatoka ofisini kwangu, na mkuu wa walinzi hapa kwenye kampuni yangu akaingia ndani.

“Una vijana wangapi hapa ofisini?”

“Wapo vijana ishirini na mbili”

“Sawa nahitaji wewe na vijana wako watatu unao waamini. Nina rudi tena vijana wako una waamini kunipatia ulinzi binafsi kuanzia hivi sasa. Umenielewa?”

“Nimekuelewa mkuu na nitahakikisha kwamba hato patwa na tatizo la aina yotote katika mikono yangu.”

“Apia mbele yangu”

“Ninaapa kwa jina la mwenyezi Mungu, nita hakikisha kwamba nina kulinda kwa uhai wangu. Nife mimi au vijana wangu ila maisha yako yabaki kuwa salama”

“Ninashukuru, hivi una itwa nani vile?”

“Mbilinyi”

“Nashukuru Mbilinyi nina kutegemea”

“Sawa mkuu. Baada ya dakika kadhaa vijana unao wahitaji watakuwa salama.”

“Haya”

Simu yangu ikaanza kuita na kukuta ni namba ya baba Camila ikitokea nchini Ujerumani. Nikaipokea simu yake.

“Ethan kuna habari nimezipata hivi sasa, kwamba umeshambuliwa kwa risasi. Ni kweli mwanangu”

“Ndio baba ila nina mshukuru nipo salama”

“Pole sana ni habari ambayo imenistua kwa kweli. Kam haupo salama sema nikutumie walinzi waweze kuja kukulinda huko”

“Hapana baba nipo salama usijali katika hilo.”

“Nimestushwa sana na habari hii hata Camila mwenyewe amestushwa sana na ameshindwa hata kuwasiliana na wewe na hivi sasa yupo hapa analia tu”

“Ohoo nipo salama baba”

“Hembu weka upande wa video nikuone”

Nikahamishia mazungumzo hayo katika upande wa video na ikawa ni rahisi kwa baba mkwe kuweza kuniona. Nikamuona baba mkwe akiwa amekaa na Camila ofisini kwake. Camila alipo niaona akafurahi.

“Upo salama mume wangu”

“Ndio mke wangu nipo salama”

“Ninakuja Tanzania sasa, sihitaji kukuacha ukiwa katika matizo. Yanai nikimaliza kuzungumza hapa na wewe nina panda ndege na kuja nchini Tanzania sawa”

Nikajikuta nikijawa na kigugumizi kizito na kushindwa hata nimjibu nini Camila kwa maana nikisema nimzuie kuja nchini Tanzania, sidhani kama baba yake anaweza kunifikiria vibaya.

“Mke wangu, kipindi hichi nilicho nacho ni kigumu, nina kuomba niweze kupambana ili nikifanikiwa basi itakuwa rahisi kwa mimi kurudi. Kumbuka kwamba wanaweza kukuteka wewe na ikawa ni kigezo kikubwa sana cha wao kunitumia mimi”

“Ethan mimi nipo vizuri mume wangu. Kwa hili haki ya Mungu ninakuja nchini Tanzania. Nakupenda sana”

Camila akaka simu hii na nikabaki nikiwa nimejawa na mshangao. Mlango wa ofisini kwangu ukafunguliwa na akaingai Biyanka moja kwa moja akanikimbilia na kunikumbatia kwa nguvu huku akilia.

“Hujaumia mume wangu?”

“Sijaumia, Mungu tu ameweze kunisaidia nimekuwa salama”

“Ohoo nashukuru jamani.”

Biyanka alizungumza kidogo akiwa amejawa na furaha. Mbilinyi akafungua mlango na kuingia na vijana wake. Wanne na jumla wakawa watano.

“Muheshimiwa vijana wangu hawa”

“Wapo vizuri”

“Sana”

“Ninaomba waweze kula kiapo mbele yangu”

Vijana hawa wakaanza kujitambulisha mmoja baada ya mwengine kisha wakaanza kula kiapo cha kunilinda kwa maisha yao yote.

“Nashukuru Mbilinyi. Hivi CCTV kamera za getini si zinafanya kazi?”

“Ndio”

“Ninaomba unitafutie video ya kipind nina shambuliwa uniletee hapa, muda huu. Walete wale vijana wawili wa IT nahitaji wafanya kazi ninayo ihitaji mbele yangu.”

“Sawa mkuu”

Mbilinyi akatoka na vijana wake hawa walio valia suti nyeusi pamoja na mashati meupe huku kila mmoja akiwa na kifaa maalumu cha mawasiliano sikioni mwake. Baada ya dakika kama nane hivi Mbilinyi akaingia na vijana wa IT wanao fanya kazi katika hii kampuni yangu. Jambo la kumshukuru Mungu kamera za getini ziliweza kurekodi kila tukio lililo tokea.

“Sura za hawa wavamizi munaweza kuzifahamu?”

“Ndio mkurugenzi”

“Fanyeni hivyo basi”

Wakaanza kufanya kazi ya kuzitambua sura za wavamizi hizi ambazo wamejifunika na mikofia myeusi. Baada ya kama robo saa hivi, vijana hawa wakafanikiwa kuzipata sura halisi za jamaa hawa. Taratibu wakaanza kuzisogeza karibu na nikajikuta nikistuka sana mara baada ya kumuona kijana wa mzee Poul Mkumbo ambaye alimuita hospalini mkoani Moshi akiwa ni miongoni mwa mtu aliye nishambulia. Nikamtazama Biyanka usoni mwake naye anaonyesha kumfahamu mtu huyo kwani ni miongoni mwa wafanyakazi wa baba yake.



Taratibu Biyanka akanishika mkono wangu wa kulia, ila nikajikuta nikiutoa mkono wake huku hasira taratibu ikianza kunipanda. Mambo aliyo niambia mama mkwe ndio haya ninayo kutana nayo hivi.

“Ninaomba muweze kutuacha”

Niliwaambia wafanyakazi wangu na wote wakatoka ndani humu na kuniacha na Biyanka.

“Huyu ni baba yako. Amepanga mpango wa kuniau si ndio”

Nilizungumza kwa hasira huku nikitazama Biyanka usoni mwake. Biyanka mwili mzima ukaanza kumtetemeka, akakosa cha kujibu.

“Kwa yale yote ambayo nimemfanyia baba yako. Huu ndio wema ambao anakwenda kunilipa si ndio”

“Ethana si….s…”

“Si si nini. Sikujua, nimepoteza muda, pesa kwa familia ambayo mwisho wanataka kunai si ndio”

Niliendelea kuzungumza kwa kofoka hadi mwili mzima ukaanza kunitetemeka kwa hasira. Katika siku zote za mahusiano yetu mimi na Biyanka sijawahi kukasirika kwa kiwango hichi.

“Baba yako anatuma majambazi waje kuniau. Kwa lipi nililo mkosea, kwa nini binadamu munakuwa watu wabaya, munakuwa wanyama kiasi hichi kwa nini lakini. Biyanka kweli unahisi nitakuoa kwa haya mambo ehee?”

“Ohoo jamani mume wangu, kumbuka hata mimi niliondoka kwa baba yangu. Ninamchukia”

“Hapana Biyanka unampenda baba yako na ataendelea kuwa baba yako. Haya akiniua ni nini amacho atanufaika nacho. Murithi malli zangu, si ndio?”

“Ethan jamani…..”

“Huo ndio ukweli. Kwakweli sinto weza kukaa kimya, sinto ruhusu uhai wangu utolewe hivi hivi ikiwa nina jua adui yangu ni nani. Hivyo ninakuomba kuanzia hivi sasa, sio mfanyakazi wa kampuni hii na mbili am out. Me and you it’s over”

Nilizungumza kwa msisitizo huku nikinguruma mithili ya simba anaye pigania familia yake isijeruhiwe na adui yake. Biyanka taratibu akapiga magoti chini huku akijaribu kunishika miguu yangu ila nikarudi nyuma.

“Ethan mimi ndio ninaye kupenda. Mimi ndo ninahitaji penzi lako. Nipo tayari kuacha kazi ila si kukuacha wewe”

“Si kuniacha mimi, so ningekufa leo ungefanya nini. Laiti kama ungefahamu kwamba ni baba yako ndio ameniua, je ungefanya nini eheee?”

Niliendelea kuzungumza kwa ukali na kumfanya Biyanka azidi kulia.

“Niambieeeee”

“NINGEMUUAAA. NINAKUAPIA NINGEMUAA BABA YANGU”

Biyanka alizungumza huku akilia sana. Nikamtazama kwa macho makali sana, yanayo endelea kububujikwa na machozi mengi sana usoni mwangu. Gafla nikaanza kuhisi maumivu makali sana moyoni mwangu, nikiwa katika hali ya kuendelea kuisikilizia hii hali mpya nikaanza kuhisi kizunguzungu kikali sana na gafla nikajikuta nikianguka chini mzimama mzima na giza totoro likaanza kutawala machoni mwangu.

“Ethaannnnnn…..Ethannn”

Niliisikia sauti ya Biyanka kwa mbali sana.

“Msaada jamani msaadaaa”

Niliendelea kuisikia sauti ya Biyanka kwa mbali sana na mwishowe nikajikuta sisikii jambo la aina yoyote.

***

Sauti ya kilio cha mwanamke, ninayo isikia karibu yangu, taratibu ikanifanya niyafumbue macho yangu. Ukungu ulio nitawala machoni mwangu, ukanifanya nisiweze kumgundua kwa haraka mwanamke huyu aliye inamisha kichwa chake pembeni yangu.

“Hei”

Niliita kwa sauti ya taratibu ambayo imejaa mikwaruzo ndani yake. Mwanamke huyu akanyanyua uso wake na nikagundua ni Biyanka.

“Baby ume amka”

Biyanka alizungumzamza huku akiwa amejawa na tabasamu usoni mwake.

“Nipo wapi?”

“Hospitali”

“Nimefikaje?”

“Ni siku sita toka ulivyo poteza fahamu mume wangu. Tumekueleta hapa nchini Afrika kusini kwa ajili ya matibabu zaidi”

“Afrika kusini, nipo hospitali gani hapa?”

“Inaitwa NetCare ni nzuri na ulinzi wake hapa ni mzuri sana”

Biyanka alizungumza kwa sauti ya upole sana huku akinitazama usoni mwangu. Nikajichunguza mwili wangua na kuona hauna tatizo la aina yoyote.

“Nina hitaji kurudi Tanzania”

“Mume wangu, ndio umezinduka sasa hivi. Huwezi kurudi nchini Tanzania hadi daktari akupe ruhusa.”

“Wamesema nina sumbuliwa na nini?”

Biyanka akaka kimya kwa sekunde kadhaa huku akionekana kujishauri shauri.

“Niambie nina sumbuliwa na nini?”

Kabla Biyanka hajanijibu jambo la aina yoyote wakaingia daktari wawili, mmoja akiwa ni mwanaume mwenye asili ya kiafrika huku mwengine akiwa ni mwanamke mwenye asili ya kizungu.

“Habari yako bwana Klopp”

“Salama”

“Mume wangu hawa ndio madaktari ambao kwa pamoja waliweza kuhakikisha wanakupatia huduma na hali yako inarudi kuwa sawa”

Biyanka aliwatambulisha madaktari hawa kwangu mimi.

“Ninasumbuliwa na nini?”

“Ahaa..ni mapema sana kuzungumza juu ya jambo linalo kusumbua bwaba Ethan ila tunakuahidi kukuambia kila jambo ambalo litakuwa lina kusumbua”

“Dokta nenda kwenye pointi ya msingi. Mimi ni mfanya biashara, kulala hapa kitandani kuna nifanya nipoteze pesa nyingi sana, wewe niambe. Ninasumbuliwa na nini na nifanye nini ili kurudi katika hali ya kawaida”

Nilizungumza kwa msisitizo na kuwafanya madaktari kujishauri kwa sekunde kadhaa.

“Bwana Klopp unasumbuliwa na mstuko wa moyo”

Macho yakanitoka huku nikiwatazama madaktari hawa. Ugonjwa wa mstuko wa moyo ni mbaya sana kwenye maisha ya binadamu kwani una weza kupelekea mgonjwa kurariki muda wowote endapo tu atashindwa kupata msaada wa karibu.

“Nina imani kwamba ni jambo jipya sana kwako na laiti kama usinge pata msaada wa haraka basi sasa hivi tungekuwa tunazungumza mambo mengine bwana Klopp”

“Ina maada maisha yangu kwa sasa yapo hatarini?”

“Siwezi kusema ndio kwa haraka haraka. Ila kuna baadhi ya mambo ambayo endapo yatafutika kichwani mwako, moja po likiwa ni kushambuliwa kwa risasi kama vile mke wako alivyo tueleza badi hali yako itakwenda kuwa sawa kabisa na utaishi miaka mingi sana. Kwani msongamano wa mawazo ambao hususani mawazo mabaya yanaweza kupelekea ukapata mshtuko wa moyo”

Daktrari alizungumza kwa msisitizo na kuzidi kuniweka katika hali ya hofu na kuogopa sana.

“Kuna dawa ambazo tutakupatia uweze kuzitumia pale tatizo litakapo kuwa linatokea hivyo zinaweza kuufanya moyo kurudi katika hali yake ya kawaida sawa”

“Sawa”

Madaktari hawa wakaniaga na kumuachia Biyanka maagizo ya kunipatia chakula kilaini laini. Kisha wao wakatoka chumbani hapa.

“Ethan usiogope mume wangu. Utaishi miaka mirefu sana kwenye hii duinia”

“Haya yote ameyataka baba yako. Unahisi kama dawa zikiwa zina nisaidia kuishi maisha marefu baba yako anaweza kunipa nafasi ya kuishi maisha hayo marefu”

“Jamani mume wangu, maswala ya baba yametokea wapi?”

“Yametokea wapi? Usijifanye nimesahau. Hizi siku nne nilizo lala hapa hizo ndio sikujua ni nini kinacho endelea, ila swala la baba yako kupanga kuniua. Linaendelea kujirudia rudia kichwani mwangu na nikitoka hapa hospitalini nina apia haki ya Mungu, nitakacho mfanya baba yako. Atafurahi na roho yake”

“Ethan nipo nawe bega kwa bega mume wangu katika hili. Nitakusaidia kuhakikisha kwamba una wakamata wale wote ambao walitumwa na baba yangu na hata baba yangu nipo tayari kuhakikisha kwamba una muangamiza kwa mikono yako”

Biyanka alizungumza kwa msisitzo wa hali ya juu hadi moyo wangu ukaanza kufarijika. Chuki ambayo nilisha anza kuipandikaza moyoni mwangu dhidi yake nayo taratibu ikaanza kuondoka. Nikakumbuka kipindi nilipo kuwa nina fanya juhudi za kuhakikisha kwamba nina mpata ili niingie kwenye familia yake na kweli kupitia penza letu nikwa mwana familia yake ninaye aminika kwa kiasi kikubwa sana.

“Huto nisaliti Biyanka”

“Nina apa haki ya Mungu sinto kusaliti na laiti kama ningekuwa ni msaliti mkubwa kwako leo hii usinge kuwepo hapa hospitali. Nimekueleta hapa hospitalini kwa siri kubwa na mtu wa pekee ambaye ana fahamu uwepo wako hapa hospitalini ni mama pamoja na Mbilinyi. Ila zaidi ya hapo hakuna mwengine anaye fahamu”

“Mbilinyi yupo wapi?”

“Yupo hapo mlangoni”

“Muite”

Biyanka akanyanyuka na kujifunga tenge lake vizuri na kufungua mlango wa chumba hichi kikubwa. Mbilinyi akaingia huku akiwa amevalia suti nyeusi. Alipo niona nipo macho kidogo uso wake ukajawa na tabasamu pana sana.

“Habari yako Mbilinyi”

“Salama mkurugenzi. Nashukuru kukuona umerudi katika hali yako ya kawaida”

“Nashukuru. Nipe update za siku hizi nilizo kata moto hapa kitandani”

“Hapa Afrika kusini hakuna jambo jipya. Usalama upo mzuri, japo nipo peke yangu ila kila jambo lipo vizuri muheshimwa. Nchini Tanzania, bado askari wanaendelea na uchunguzi wao ni nusu saa lililo pita nilikuwa nina zungumza na kijana wangu mmoja, anadai hadi sasa hivi hakuna aliye kamatwa”

“Ule ushahidi muliweza kuwapatia askari?”

“Hapana, hatukuweza kuutoka hadi pale utakapo zungumza tuutoe”

“Wala musiutoe, nikapata ruhusa hapa nitajua ni nini cha kufanya sawa”

“Sawa mkurugenzi”

“Nashukuru bwana kwa kuendelea kuwa nami kwenye shida na raha.”

“Ni jukumu langu mkurugenzi. Nilikula kiapo cha kuhakikisha nina kulinda kwa uhai wangu”

“Nashukuru sana, sawa unaweza kumsindikiza shemeji yako kutafuta chakula kizuri”

“Ila muheshimiwa utakuwa mwenyewe hapa hospitalini”

“Hakuna taba ikiwa nimesha weza kuamka na kidogo nina jisikia vizuri basi hakuna ambaye anaweza kunivamia”

“Ila mume wangu ninaweza kwenda tu mwenyewe”

“Wewe nenda na Mbilinyi. Hapa ndani ni salama kuliko hata huko nje ambapo munahitaji kwenda”

“Sawa”

Biyanka alikubaki kishongo upande akanipiga busu la mdomoni mwangu kisha wakatoka ndani hapa na kuniacha peke yangu.

“Nimekupa nafasi ya kufanya kama ulivyo niomba ufanye. Mwisho wake umeishia hospitali”

Ethan alizungumza huku akiwa ameegemea mlango. Taratibu akaanza kutembea na kusimama pembeni yangu, akanishika kifuani mwangu na mkono wake wa kushoto, nikasikia ubaridi mkali sana na hali ya mwili wangu ikarudi kawaida kama siku zote.

“Nilkuwea kaugonjwa haka ka mstuko wa moyo ili uweze kugundua kwamba mimi na wewe hatupo sawa na utambue, kutokea utoto hadi tunafikia hapa ni mimi ambaye nimekupa nafasi na nguvu kubwa katika jamii. Hivyo siku nyingine usijaribu kunijibu kwa akili zako za kibinadamu kwa maana niyakupoteza duniani. Umenielewa?”

Ethan alizungumza kwa msisitizo huku akinikazia macho.

“Nimekuelewa”

“Wakirudi omba madaktari wakupime tena. Majibu yatatoka huna ugonjwa wowote na urudi nchini Tanzania na ukaendelee na mapambano. Nakurud kukuambia, vita ambayo unahisi uliifanya hapo nyuma, zile zilikuwa ni rasha rasha tu. Sasa vita halisi ndio kama hiyo ambayo unakutana nayo. Macho kwa macho, mtutu kwa mtutu. Sijui umeelewa kile nilicho kizungumza?”

“Nimekuelewa”

“Alafu nina habari ambayo sio nzuri sana”

“Habar gani?”

“Juzi mke wako Camila alivyo kuwa ana fika nchini Tanzania, kwa bahati mbaya ndege ambayo walikuwa wameipanda ilipata ajali na kuanguka hapo hapo uwanjani”

“What….!!!”

“Tulia, Camila amevunjika tu mkono na majeraha madogo madogo ya kuchubuka. Ila abiria zaidi ya mia na tisini walipoteza maisha”

“Weee sasa ni nini chanzo cha ajali?””

Ethan akawasha tv iliyomo humu chumbani. Akaweka chanel inaoyo rusha habari juu ya ajali hiyo ya ndege. Nikaona picha mbili, mtu mmoja nina mfahamu vizuri. Ni mtoto wa Dany ambaye anaitwa Randy Dany na huyu mwanamke simfahamu kabisa.

“Hao ndio walio sababisha ajali hiyo. Wanaendelea kutafutwa kwa udi na uvumba na nchi kama Marekani pamoja na Ujerumani wametuma wapelelezi wao kuhakikisha wanaongeza nguvu juu ya kukamatwa kwa watu hao. Inavyo semekeana mke wake huyo Randy ame waua rubani wawili wa ndege ambayo walikuwa wameipanda.”

“Mmm hayo mambo yamekuwaje kuwaje hadi kufika hapo?”

“Yamekuwa kama hivyo yalivyo kuwa. Kikubwa ni kumshukuru Mungu mke wako yupo salama”

“Kwa sasa yupo wapi Camila?”

“Yupo katika ubalozi wa Ujerumani nchini Tanzania”

“Sasa hao walio sababisha hayo mauaji ya abiria wote hao. Wewe hujui ni wapi walipo?”

“Natambua ni wapi walipo”

“Sasa wasaidie basi serikali wakawakamate”

“Siwezi, kufanya hivyo. Tupambane na hali zetu hizo hali za wengine tuwaachie wengine wapambane na hali zao”

Ethan mara baada ya kuzungumza maneno hayo akapotea ndani ya chumba changu na kuniacha nikitazama habari hii inayonyesha jinsi ndege hiyo inavyo gongana na magari kadhaa ya askari na kupoteza muelekeo wake na mwisho kuanguka.



Mlango ukafunguliwa na Biyanka akaingia akiwa ameshika mfuko mweupe wenye mandishi yenye rangi ya kijanni. Akatazama taarifa hiyo ya habari ninayo ifwatilia kisha akachukua rimoti na kuzima tv.

“Mbona una zima sasa tv?”

“Sio habari ya kuitazama muda huu mume wangu. Nahitaji uweze kupata chakula sasa”

“Ahaa…hembu washa bwana”

“Ethan nina tambua kwamba unahitaji kufahamu mambo mengi sana yanayo endelea nchini Tanzania, ila nina kuomba kwanza utulie. Usije ukapata mstuko wa moyo tena na ukasababisha matatizo mengi”

“Sina tatizo hilo”

“Kivipi tena mume wangu”

“Nimekuambia sina tatizo tena la mstuko wa moyo, hao madaktari wako wamekosea vipimo vyao”

Biyanka akatabasamu huku akinitazama usoni mwangu.

“Mme wangu acha masihara bwana”

“Ninacho kuambia ni jambo la ukweli, waite madaktari wako wanipime waone kama nina tatizo la moyo. Mambo ya kutiana presha presha za kipuuzi sipendi mimi”

“Mume wangu ina maana upo serious?”

“Ndio maana yake”

Biyanka akanitazama jinsi nilivyo jawa na msisitizo. Akasogelea meza iliyopo karibu yangu na kunyanyua mkonga wa simu hii ya mezani. Akaminya batani kadhaa kisha akaiweka sikioni mwake.

“Ndio, VIP 02 nahitaji madaktari wangu”

“Nashukuru”

Biyanka akarudisha mkonga wa simu katika sehemu aliyo itoa na kunitazama usoni mwangu.

“Ethan hali yako imebadilika tofauti na pale nilipo kuacha hem…..”

“Ndio imebadilika nimerudi katika hali yangu ya kawaida. Nimekuambia kwamba siumwi mimi”

“Hapana sio kama huumwi ila naona kama kuna tatizo jengine jipya lililo jitokeza. Samahani lakini kama nitakuwa nina kuudhi. Naona kama akili zako zimekuruka vile”

Macho yakanitoka huku nikimtazama Biyanka aliye anza kurudi nyuma nyuma huku akionekana kunishangaa sana.

“Kwa hiyo sasa hivi mimi nimerukwa na akili si ndio?”

Madaktari wakaingai ndani humu. Wote wakabaki wakiwa wamejawa namshangao baada ya kunikuta nikiwa nimeshuka kitandani.

“Bwana Klopp una nguvu za kusimama?”

“Ndio kwani nilivunjika. Hembu rudieni vipimo vyenu vya kunipima nina hitaji kuondoka hapa hospotalini”

“Bwana Klopp ila inabidi uweze kupata mda kidogo wa kutulia ili mwili urudi kwenye hali ya kawaida”

“Oya dokta sentensi yangu ya awali hujaweza kuisikia au? Nimekuambia kwamba nahitaji munipime kama nina tatizo la moyo, nitakubali kurudi kitandani, ila kama sina tatizo la moyo niruhusu niweze kuondoka hapa. Munahisi nina furahia mimi kuendelea kukaa hapa kama mzigo”

Madaktari hawa wakatazamana kwa sekunde kadha kwa maana nina zungumza kwa msisitizo mkali sana. Wakakubaliana na mimi, tukatoka katika chumba hichi na moja kwa moja tukaelekea hadi kwenye moja chumba cha vipimo. Wakaanza kunipima vipimo vyote hususani vya moyo ambao waliniambia una matatizo.

“Heee hana ni ajabu sana”

Madaktari hawa walizungumza huku wakiendelea kujawa na mshangao mkubwa.

“Kweli?”

“Ndio hana tatizo”

“Imekuwaje?”

“Hata mimi sifahamu dokta sijawahi kuona kitu kama hichi”

“Munegundua kwamba sina tatizo ehee?”

“Ahaa…ndio bwana Ethan”

“Basi muelewe kwamba muda mwengine mgonjwa anavyo zungumza kwamba hana tatizo muwe muna muelewa na si kuamini majimashine yenu haya. Munatuadai kiasi gani?”

“Bili yote ya hospitalini nimesha lipa mume wangu”

“Kwahiyo hatudaiwi?”

“Ndio”

“Sawa tuondoke”

Nilizungumza huku nikitangulia kutoka ofisini humu na kumkuta Mbilinyi akiwa amesimama mlangoni.

“Mkurugenzi vipi?”

“Nipo poa. Inabidi tujiandae turudi Tanzania leo hii hii”

“Sawa mkuu unahitaji niandae mazingira ya usiri ya wewe kurudi Tanzania, au niache watu waweze kukuona?”

Nikajifikiria kwa sekunde kadhaa huku nikimtazmaa bwana Mbilinyi usoni mwake.

“Yawe ya siri”

“Sawa mkuu”

Bwaana Mbilinyi akatoa simu yake mfukoni na kuanza kuwasiliana na watu ana watambua yeye mwenyewe. Biyanka akatoka katika chumba hicho huku akiwa ameshika faili mkononi mwake.

“Nina furaha kuona mume wangu umerudi katika hali yako ya kawaida. Nina omba uweze kunisamehe kwa pointi ya kukuambia kwamba ume changanyikwa”

“Usijali, ehee tunaondoka na ndege gani?”

“Inabidi tulale hotelini kwanza mume wangu kisha ndio tutarudi nchini Tanzania”

“Hotelini tena, ikiwa nina taka kupanda ndege sasa hivi na kuondoka nchini hapa”

“Hapana mume wangu, hemu nina kuomba basi uvumilie kidogo. Nahitaji kuhakikisha kwamba tunaondoka nchini hapa tukiwa na faida kubwa. Kuna wafanya biashara wa kubwa wanao dili na mambo ya mitandao ya mawasiliano, hivyo tukionana nao nina imani kwamba tunaweza kuutanua zaidi mtandao wetu wa simu na kujikuta tukiendelea kupata pesa nyingi nyingi sana ambazo zitazidi kutukuza kiuchumi”

Maneno ya Biyanka kidogo yakaniingia akilini, kwa maana katika swala la pesa hakuna tajiri ambaye ana ikataa, hata kama ana miliki kiwango kikubwa cha pesa ila ni lazima atahitaji kukiongeza mara dufu.

“Wana pesa lakini?”

“Mume wangu tambua kwamba mimi nime base kwenye mambo haya ya hii biashara, natambua faidi na hasara ambayo tutahitaji kuitengeneza na siwezi kukupeleka kwa watu ambao hawana pesa. Lazima tupate pesa nyingi sana mume wangu na isitoshe tumepoteza pesa nyingi kwenye kipindi hichi cha uchaguzi hembu tuangalie jinsi gani tunaweza ku fix ishu hiyo ya pesa”

“Sawa. Ehee alafu baadae nikumbushe nikuambie kitu”

“Kitu gani?”

“Baadae wewe ni kumbushe”

“Sawa, twende basi chumbani ukavae ubadilishe hizo nguo za hospitalini”

Tukarud katka chumba ambacho nilikuwa nimelazwa. Biyanka akanitolea nguo mpya alizo ninunulia, siku ambayo siifahamu. Nikazivaa,, tukachukua kila kilicho chetu kisha tukaondoka hospitalini hapa huku nikiwa nimevalia miwani pamoja na kofia ili watu au waandishi wa habari wasiweze kunifahamu kwa haraka kwa maana umaarufu wangu si Ujerumani au Tanzania pekee bali ni karibia dunia nzima.

“Kumbe nchi hii imejengeka nayo ehee?”

Nilimuuliza Biyanka huku nikitazama tazama magorofa kadhaa yanayo fanania na magorofa yaliyopo nchi za bara la Ulaya au Asia.

“Yaa imejengeka kwa kweli, hii watu wa Tanzania wenyewe wanaipaita ulaya ndogo”

“Hahaa kweli ni ulaya ndogo, naona wazungu wapo wengi wengi”

“Yaa huku wamechanganyika na waafrika.”

“Hivi hii ndio ile nchi ya Mandela ehee?”

“Yaa kwani hukuwahi kufika katika nchi hii?”

“Hapana kwa kukaa kwangu kote Tanzania, sijawahi kufka nchini hapa”

“Basi ni sehemu nzuri sana mume wangu”

Biyanka alizungumza huku akiwa amejawa na furaha. Taratibu akakiegemesha kichwa chake katika bega langu la upande wa kulia.

“Mbilinyi mbona upo kimya?”

“Hapana mkuu, nina wapa nafasi muzungumze na madam hapo kwa maana siku kadhaa zilizo pita hakuwa katika hali kama hiyo ya furaha”

“Wee alikuwaje?”

Mbilinyi akageuka nyuma na kunikabidhi simu yake. Nikaona video aliyo irekodi Biyanka akinililia kwa uchungu sana huku akimuomba Mungu.

“Wee Mbilinyi kumbe ulinirekodi jamani?”

“Yaa nilifanya hivyo ili iwe kama ushuhuda, kwa mkurugenzi hapo na watu wengi kama wakihitaji kujua ni mateso gani ambayo uliyapitia kipindi mkurugenzi ana umwa”

Mbilinyi alizungumza kwa furaha huku dereva wa gari hii walilo kodisha akiendelea kutuendesha kwa mwendo wa kawaida.

“Ila mke wangu ulilia hadi umekuwa mwenkundu”

“Jamani?”

“Ndio ona hapa ulivyo kuwa mwekundu”

“Ila mkurugenzi unajua ni nini?”

“Sijui niambie”

“Tanzania kuna wanawake wa kuoa na wanawake wa kuchapa ilale, samahani kwa kutumia msemo huo. Ila kusema kweli niwe muwazi mke wako ana kupenda sana, mke wako ana kuthamini, alikuwa hali, wala anywi. Mule chumbani kwa mara kadhaa nilikuwa nina ingia nina mkuta akiwa amepiga magoti akisali, vyakula nilvyo kuwa nina mletea alikwa ni mtu wa kuvitupa tu kwenye dastebin. Ilifikia hatua nikawa na wasiwasi, nikawa nina jiuliza je ikitokea umelala mwezi mzima kitandani si tutampoteza na yeye”

Maneno ya Mbilinyi yakanifanya nimtazame Biyanka usoni mwake. Yakanifanya nijawe na huzuni pamoja na imani kubwa sana, nikamfungua Biyaka kitenge chake alicho kizungushia kifuani mwake, sikuamini nilipo muona maeneo ya shingoni jinsi alivyo anaza kubonyea kutokana na kukonda.

“Mkurugenzi hakika hapo una mke wa kuoa. Katika wanawake mia moja, kumpata mtu kama madam hapo labda ni mmoja ana wawili. Aliweka pembeni utajiri wake aliweka pembeni cheo chake, alijishusha mbele za Mungu na kumlilia kila siku, hakujali kama hospitali au madaktari walipo wanaweza kukuokoa, ila alilia kwa ajili yako. Kuna muda hata mimi aliniliza japo ni jasiri ila kwa hali ambayo alikuwa nayo hakika aliumia sana”

Mbilinyi alizungumza maneno ambayo yalianza kumfanya Biyanka kumwagikwa na machozi. Huruma na upendo wangu ambao kidogo ulianza kujawa na mashaka dhidi ya Biyanka vikaanza kuchanua taratibu. Tukafika hotelini na tukashuka kwenye gari hili, tukapitiliza hadi kwenye lifti.

“Mbona dereva hamja mlipa?”

“Tulisha lipa kampuni yao hivyo ana tupelekea popote tunapo taka. Kama kutakuwa na kiasi chochote kilicho zidi basi tutakiongezee”

Mbilinyi alizungumza huku akiminya batani ya lifti tuliyo ingia. Biyanka hakuzungumza kitu chochote zaidi ya kuung’ang’ania mkono wangu huku uso wake akiwa ameuelekeza chini. Lifti ikafika katika gorofa ya ishirini na mbili na tukatoka katika lifti hii na kuanza kutembea katika kordo hii ndege.

Mbilinyi akatoa kadi ya kufungulia mlango huu, baada ya kufungua mlango akawa mtu wa kwanza kuingia ndani kuhakikisha kama kuna jambo lolote bada basi ataweza kutulinda. Katika eneo hili kuna seble kubwa pamoja na milango mingine miwili iliyopo katika hii korodo.

“Kuna vyumba viwili?”

“Ndio mkuu”

Biyanka akanishika mkono, tukatembea hadi kwenye chumba kimoja ambacho kwa ndani ni kikubwa na kina kitanda kizuri. Biyanka akanikumbatia kwa nguvu na kuanza kuangua kilio cha furaha.

“Ethan nina kupenda sana mume wangu. Nisamehe kwa kila jambo lililo tokea kwenye famila yangu”

Biyanka alizungumza huku taratibu akianza kupiga magoti, kabla ya kufika chini nikamuwahi kumnyanyua.

“Unataka kufanya nini mke wangu”

Nilizungumza huku machozi yakinilenge lenga kwa maana unyenyekevu huu anao endelea kuufanya Biyanka kwangu, hakika hata uwe ni mwanaume wa aina gani lazima utakuwa mpole kwake.

“Haya yote ameyataka baba yangu. Laiti ingekuwa sio yeye basi haya yasinge tokea. Ethan moyo wangu ulizidi kujawa na uchungu sana pale nilipo kuona kitandani. Niltamani sana kukuamsha japo ule na mimi, japo ucheke na mimi ila sikuweza kufanya hivyo. Nilumia mume wangu na niliteseka, niliapa kufa pale tu utakapo kufa. Ila Mungu wa mbinguni ametenda tena muujuza wake. Nakuomba sana mume wangu isamehe familia yangu, hata mwenye amekuwa akilia, akifunga na kusali kuhakikisha kwamba unarudi kwenye hali yako ya kawaida na kweli Mungu amejibu maombi yetu”

Biyanka alizungumza kwa upole na unyenyekevu sana huku akiwa ameishia mikono yangu.

“Ethan, nimeamua maisha yangu kumkabidhi Mungu. Nimepitia maisha mengi mabaya nyuma, nimefanya vitu vibaya, vingine vikiwa kwa kupenda huku vingine vikiwa kwa kufundishwa na baba yangu. Ila nilipiga goti mbele za Mungu na kumuomba msamaha, nilipiga goti kuhakikisha kwamba Mungu ananisamehe yale yote niliyo fanya na ninamshukuru Mungu amezidi kusikia kilio changu na hata ule ugonjwa wako wa moyo niliupelekea mbele zake na akafanikiwa kuutoa. Hakika Mungu ni mkubwa, nina kuomba sana Mume wangu naomba umkabidhi Mungu maisha yako, tafadhali mume wangu”

Biyanka alizidi kuninyenyekea huku mashavu yake yakiendelea kujawa na machozi.

“Nitamkabidhi maisha yangu ila kwa sasa bado”

“Ethan kwenye kumpa maisha yako hakuna kesho. Amua sasa mume wangu, tuende mbele za Mungu na tutubu dhambi zetu”

“Biyanka bado siwezi kuokoka sasa hivi. Nitaokoka mara tu baada ya kuhakikisha kwamba ninampokonya baba yako kila kitu alicho kichukua kwenye maisha yangu na nilazima alipe kwa vifo vya alivyo wafanyia wazazi wangu kipindi nipo mtoto”

Nilijikuta nikitoa siri ambayo Biyanka toka aanze mahusiano na mimi hakuwahi kuisika wala kuhisi kwamba nyuma yangu kuna siri kubwa kama hiyo ambayo endapo ataifafanua vizuri kichwani mwake lazima ataelewa kwamba mambo yote mabaya yaliyo tokea kwenye familia yake mimi ndio chanzao kikubwa na ndio niliye pelekea familia hiyo kusambaratika kwa sasa.



“Alikuulia wazazi wako!!?”

Biyanka alinuuliza huku akiwa amejawa na mshangao mkubwa snaa usoni mwake.

“Ndio aliwapiga risasi na niliwashuhudia kabisa akiwaangamiza. Siwezi kumsamehe kabisa baba yako”

Biyanka akabaki na mshangao huku akionekana kutamani kuzungumza jambo fulani ila anashindwa kutokana na kigugumizi kikali alicho kipata.

“Baba yako ni adui yangu namba moja na nilihakikisha kwenye maisha yangu nina tafuta nguvu kuhakikisha kama ni kupambana naye basi nitapambana naye kikamilifu, hadi niakikishe kwamba ana shuka ana shuka na kuwa masikini mkubwa kama alivyo pokonya madini ya baba na mama yangu”

“Ethan unataka kuniambia kwamba ule mgodi ni wa baba yako?”

“Lile eneo ni la baba yangu. Ila umasikini wa baba yangu na kuto kuwa na nguvu ya pesa aliweza kumdhulumbu ni bora hata angemuacha hai tukaendelea kuteseka na maisha haya ila alikwenda mbali zaidi na kuwaua, tena usiku, mvua ikinyesha huku radi zikiwa zimetanda angani. Niliogopa sana, na vijana wake akiwemo yule aliye nishambulia kwa risasi, walimbaka mama yangu mbele yangu na kwenda kunitupa kwenye maporomoko yaliyopo eneo lile la mgodini. Waliamini kama nimekufa, walijua kwamba nime angamia ndio maana hadi leo baba yako ana tawala na kumiliki ule mgo bila ya bugza yoyote. Heee nipo hai mama na nitarudisha kila kilicho changu alicho nipokonya”

Nilizungumza huku machozi yakini mwagika usoni mwangu. Biyanka akabaki mdomo wazi, taratibu akanishika mkono na tukaka kitandani kwa upole.

“Ethan, kwa nini hukuniambia hayo yote ikiwa tulikuwa tukishirikiana kila jambo”

Biyanka aliniuliza kwa sauti ya upole huku naye machozi yakimwagika usoni mwake.

“Unahisi kwamba ungeniambia ukweli leo hii ningekuwa naye. Leo hii ningekuwa nina pumua hapa duniani. Leo hii ningekuwa nimewekeza nchini Tanzania?”

Nilizungumza kwa uchugu huku nikiendelea kumtazama Biyanka ambaye amekuwa mnyonge na mpole sana.

“Baba yako angekuwa raisi unahisi ningeweza kupambana naye vipi ikiwa ana mamlaka ya kila aina. Nilihakikisha kwamba baba yako haikanyagi ikulu, sikuumia kupoteza pesa zangu kwa ajili ya kuhakikisha ana kosa cheo hicho na nina mshukuru Mungu baba kwamba nimefanikiwa katika hilo”

Nilijikuta nikitoboa siri nyingine ambayo si rahisi kwa Biyanka kuweza kuniamini kwa haraka haraka kwa maana jinsi nilivyo kuwa nina hangaika juu ya kuhakikisha kwamba baba yake ana ingia madarakani kwa nanma yoyote ile.

“Ethan ni wewe?”

“Ndio ni mimi na bado nipo kwenye mapambano ya kuhakikisha kwamba baba yako anarudisha kila kitu”

Biyanka akashusha pumzi nyingi huku akinitazama usoni mwangu.

“Yaani siamini kwa hili la sasa hivi unalo niambia mume wangu”

“Niamini, je nahitaji kujua kwamba upo na mimi au haupo na mimi kwenye huu mpango?”

“Ethan nilisha kueleza kwamba nipo na wewe katika kila jambo. Mim ni nipo tayari katika hili, ila nakuomba jambo moja uweze kunikubalia”

“Siwezi kukubalia kama bado sijaweza kulifahamu hilo jambo lenyewe”

“Nina kuomba usimuue baba. Sihitaji dhambi ya damu yake iwe juu ya familia yetu hususani kwa vizazi vyetu. Kumbuka tutakuwa na watoto, je wakija kufaamu kama wewe na baba mulikuwa na uadui na wewe ukachukua maamuzi ya kumuua baba unahisi ni kitu gani ambacho kinaweza kwenda kutokea hapo?”

Nikaka kimya huku nikimtazama Biyanka uson mwake.

“Mume wangu, sikukatazi kufanya hayo uliyo yapanga kuyafanya kwa baba kwa maana ni mambo uliyo yakusudia kutoka moyoni mwako. Ila swala la kumuua tu ndio ninaomba uweze kumsamehe sawa baba aangu”

“Sawa mke wangu, ila kwa ajili yako nitampa msamaha ila nina kuomba kwamba usinisaliti katika hili umenielewa”

“Siwezi kufanya hivyo mume wangu”

“Kweli?”

“Kweli nakuapia kwa jila la mwenyezi Mungu wangu ninaye muamini hivi sasa siwezi kufanya hivyo mume wangu”

“Nashukuru na nina furahi kusika hivyo”

Biyanka akanikumbatia kwa nguvu na kunifanya nianze kulisikilizia joto lake lililo anza kunyanyanyua hisia zangu za kimapenzi. Nikaanza kumshika Biyanka kiuno chake kwa hisia kali sana, taratibu Biyanka akanishika mkono wangu na kuusogeza pembeni.

“Mume wangu nakuomba uweze kunivumilia”

Biyanka alizungumza kwa sauti ya upole na iliyo jaa ungenyekevu ndani yake.

“Kwa nini?”

“Nipo kwenye kipindi cha mfungo wa maombi kwa wiki hii nzima. Nakuomba sana uweze kunivumilia, mume wangu”

“Usijali”

“Tafadali mume wangu, sijakataa kukupa tendo la ndoa. Ila nielewe tu kama nipo kwenye mfungo wa maombi juu ya familia yetu kwa maana endapo asipo tokea mtu wa kusimama kwa ajili ya maombi ya hii familia hakika wote tutakwenda kuteketea”

“Sawa mke wangu nimekuelewa acha nikaoge”

“Haya na wale wafanya biashara ngoja niwasiliane nao ili ikiwezekana tuonana nao kesho asubuhi kwenye hii hoteli”

“Haya”

Nikanyanyuka kitandani nilipo kaa na kuingia bafuni. Nikavua nguo zangu na kusimama kwenye kioo kikubwa kilichopo humu ndani. Nikajitazama mwili wangu na kuuona jinsi ulivyo pungua kwa siku hizi kadhaa ambazo nimekaa hospitalini. Nikaoga kisha nikarudi chumbani na kukuta Biyanka akwia amesha niandalia nguo za kuvaa.

Nikavaa na kutoka ndani humu na kuwakuta Biyanka na Mbilinyi wakiwa sebleni wakekaa.

“Ndio mkurugenzi”

“Ehee vipi ulisha zungumza na vijana wako?”

“Ndio mkuu kila kitu kipo sawa.”

“Mume wangu nimepokea moja ua email kutoka katika kocha wa timu ya Real Madrid ya Spain anaomba niweze kukuunganisha kwako”

“Amekujuaje?”

“Sijajua ila ni email ambayo imeingia muda huu hapa, chukua uisome”

Biyanka akanikabidhi simu yake na nikaipitia email hii na kweli inatoka kwenye klabu kubwa ya mpira hapa duniani ya Real Madrid.

“Hembu zinakili hizo namba za simu kisha wapigie nizungumze nao”

“Sasa hivi?”

“Ndio”

Biyanka akazinakili namba hizo kisha akabidhi simu niweze kuzungumza na kocha huyo. Simu ikaanza kuita na baada ya muda kidogo simu ikapokelewa.

“Unazungumza na bwana Ethan Klopp.”

Nilizungumza kwa lugha ya kifaransa.

“Ohoo nashukuru kukufahamu bwana Klopp niliweza kupewa email ya mke wako hivyo nilimtumia meseji ili tuwasiliane”

Kocha huyo alizungumza kwa lugha ya kifaransa.

“Sawa ninakusililiza kocha”

“Ninahitaji kuweza kukusajili katika dirisha kubwa msimu ujao je tunaweza kufanya mazungumzo ya uso kwa uso”

“Ndio tunaweza kuzungumza na kwa sasa nipo nchini Afrika kusini”

“Kama upo Afrika kusini basi ninapanda ndege binafsi na nina imani kesho nitakuwepo katika nchi hiyo”

“Sawa muheshimiwa ukifika utawasiliana nami kwa namba hii”

“Nashukuru sana bwana Klopp”

“Nami pia nina shukuru”

Nikakata simu na kumkabidhi Biyanka.

“Unataka kuanza kucheza mpira mume wangu?”

“Ndio nikimaliza kila jambo nina imani utakuwa ni muda wangu mzuri wa mimi kuweza kucheza mpira”

“Mkurugenzi nilifanikiwa kutazama clip zako za miaka kadhaa iliyo pita hakika upo vizuri sana”

“Nashukuru”

Usiku wa siku ya leo tukaelekea katika mgawaha mkubwa uliopo ndani ya hii hoteli na kuanza kupata chakula cha usiku huku tukiwa ni watu walio jawa na furaha sana. Machozi na huzuni vimefutika kwa mke wangu.

“Mkurugenzi”

“Naam”

“Unaonaje ukirudi nchini Tanzania mukafunga pingu za maisha ya madam hapo?”

“Ahaa huo mpangoupo Mbilinyi. Ila kuna haya mambo ya mzee huyu nikiyamaliza basi nitafunga bonge moja la ndoa ambalo nina imani nyinyi nyote muta furahia”

“Itakuwa baraka na furaha kwenu. Unajua Mungu amewabariki kika aina ya mali ya duniani munayo. Ila nina imani kwamba furaha yenu ita kamilika pale tu mutakapo pata mtoto. Hakika nina imani mutakuwa ni watu wenye furaha zaidi ya hii muliyo nayo hivi sasa”

“Mume wangu anacho kizungumza Mbilinyi ni kweli”

“Sawa tutalifanyia kazi mke wangu”

Tulipo maliza kupata chakula cha usiku tukaondoka ndani hapa na kurudi chumbani na kulala. Asubuhi na mapema tukaingia kwenye mkutano na wafanya biashara wanao miliki mitando ya mawasiliano hapa nchini Afrika Kusini na kuanza kufanya nao mazungumzo ya kibiashara ambayo yakaishia kwa mapatano ya kushirikiana katika maswala ya kibiashara.

“Kazi nzuri mke wangu”

“Nashukuru mume wangu”

“Sikutarajia kama kikao kitaishia hivi, umejitahidi “

“Asante na hapa kuna ofa nyingine ambayo nime ipata”

“Kutoka wapi?”

“Katika kampuni moja ya watengenezaji wa simu. Wanahitaji waweze kututengenezea simu zenye jina la kampuni yetu na tutakuwa tunagawana nao asilimia tutakayo kubaliana katika mauzo yote”

Nikajikuta nikimkumbatia Biyanka kwa furaha kubwa sana huku moyoni mwangu nikitamani kumueleza siri ambayo hakuwahi kuijua kabisa kwenye maisha yake.

“Nisamehe mke wangu”

“Nikusamehe na nini?”

Nikashusha pumzi huku nikimuachia tararibu, nikatamani kumueleza kwamba yeye kwangu ni mke wa pili na juhudu hizi zote anazo zifanya yupo mwanamke ninaye mpenda sana kulilo yeye.



ENDELEA

“Kwa kila jambo baya nililo lifanya bila ya wewe kufahamu”

“Mume wangu, tambua Mungu ndio anaye tambua ukweli wa kila moyo wa binadamu. Nimekusamehe mume wangu na nipo nawe baga kwa bega katika maisha yangu”

Jioni ya siku ya leo nikakutana na kocha wa timu ya Real Madrid katika mmoja wa mgahawa ulipo katika nchi hii. Mbilinyi hakuwa mbali sana ili kuhakikisha kwamab ana tulinda na jambo lolote baya ambalo linaweza kutokea.

“Huyu ni mke wangu anaitwa Biyanka”

“Nashukuru kukufahamu Biyanka nilikuwa nina kuona kwenye picha tu”

“Nashukuru kukujua na wewe kocha”

“Sawa ninaweza tukapata muda sisi wawili tukazungumza?”

“Ohoo hakuna tatizo acha niwapishe”

Biyanka akanyanyuka na kuhamia katika meza ya pembeni.

“Bwana Ethan acha niende kwenye point ya kukutana kwetu. Ninahitaji urudi kiwanjani, nimekuwa nikikuona tasa kwenye mipango yangu toka kipindi kile ulipo kuwa unashiriki yale mashindano ya kishule. Una kitu ambacho wachezaji wengi hawana na kitu hicho ni maalumu sana, hata ukikaa nje ya uwanja kwa miaka kadhaa hakito weze kupotea wala kushuka. Hivyo nakusikiliza wewe kama upo tayari kuwa miongoni mwa wachezaji katika kikosi changu”

Nikaka kimya kwa sekunde huku nikimtazama kocha huyu.

“Uliniambia una hitaji nijisajili katika kikosi chako kwa msimo ujao?”

“Ndio”

“Ofa yenu ipo vipi kwa manaa wewe katika timu yako una master wengi sana. Je nitapata nafasi ya kucheza?”

“Ndio nafasi ya kucheza lazima uipate Ethan. Ndio maana nikafunga safari kutoka Spain hadi hapa Afrika kusini kwa ajili yako”

“Sawa, nimekuelewa nipo tayari ila kwa masharti mawili au matatu hivi”

“Ehee nayasikiliza”

“Nahitaji kuwa mchezaji anaye lipwa pesa nyingi mara nne ya kiwango anacho lipwa mchazaji anaye ongoza kwa kipato hicho kwa sasa hapa duniani”

“Hilo halina shida kwa maana hutajakusajili kutoka katika timu yoyote basi tunaweza kufanikisha huo mshahara”

“Sawa. Sharti la pili endapo nitaitwa katika timu yangu ya Taifa ya Tanzania, nitahitaji niweze kushiriki kwa nguvu zote”

“Ngoja kwanza ina maana huto chezea timu ya taifa ya Ujerumani?”

“Mimi ni Mtanzania na nitacheza timu ya taifa ya Tanzania”

“Sawa hilo linawezekana. Jengine”

“Shatri la tatu, nitahitaji mshahara wangu usihusiane na kodi yaa ina yoyote katika nchi ya Spain kama ni kodi hiyo ya mishahara basi ikatwe katika timu ila si mshahara wangu”

“Hilo nalo linawezekana.”

“Kama yana wezekana basi mimi nipo tayari kujiunga na timu yako”

“Nina imani nitategemea mambo makubwa zaidi ya haya”

“Ndo”

“Nashukuru sana bwana Ethan na nina furaha kubwa sana. Niandikie muda wowote email na kama inawezekana uweze kurudi uwanjani mapema kabisa kwa maandalizi”

“Usijali”

Tukamaliza mazungumzo haya na huyu kocha kisha tukaagana na kuondoka katika mgahawa huu na kurudi hotelini.

“Mume wangu inabidi uanze mazoezi ya mpira unajua mpira una hitaji maandalizi”

“Yaa tukirudi nchini Tanzania, nahitaji kununua eneo ambalo nitajenga kiwanja kikubwa cha mpira ambacho timu nitakayo ianzisha basi inaweza kwenda kufanya mazoezi”

“Sawa ni wazo zuri pia mume wangu, nitakuunga mkono”

Siku za kukaa nchi hapa Afrika zikaisha. Tukapanda ndege na kuianza safari ya kurudi nchini Tanzania kimya kimya huku vijana wa Mbilinyi wakiwa wamejiandaa kutupokea katika uwanja wa mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.

“Inabidi tukifika Tanzania usionekana hadi pale tutakapo jua hali halisi ya nchi ina kwenda vipi”

Biyanka alizungumza kwa kuninong’oneza huku akiwa pembeni yangu.

“Usijali mke wangu. Pina nina mpango wa kununua nyumba”

“Ya aina gani au kwa nini usijenge nyumba ambayo una ihitaji wewe mwenyewe?”

“Lipi bora kununua au kujenga?”

“Bora ujenge”

“Ila nyumba ninayo ihitaji ni ya siri sana ambayo baba yako hato weza kujawa na mawazo ya kwamba mimi nina weza kuishi kwenye nyumba kama hiyo. Kama hapa tukisema twende kwako moja kwa moja inaweza kuleta shida”

“Mmmm ila ni kweli”

“Hapa inabidi nifikizie nyumbani kwa Mbilinyi na nyumba ikipatikana basi nitahamia”

“Nyumbani kwa Mbilinyi…Hapana tufikirie sehemu nyingine”

“Hotelini mimi siwezi kufikizia na Mbilinyi na wewe ndio watu nina waamini kwa hivi sasa”

“Ngoja tufike tutajua ni kitu gani kilicho andaliwa.”

Majira ya saa sita usiku tukafika jijini Dar es Salaam. Tukawakuta vijana wa Mbilinyi wakiwa wametengeneza mazingira ambayo hakuna muandishi wa habari anaweza kufahamu. Tukaingia kwenye gari na safari ya kuondoka eneo hili likaanza.

“Nyumba muliyo iandaa ni salama?”

“Ndio mkuu ni salama kabisa”

Kijana wa Mbilinyi anaye endesha gari hili alizungumza huku gari jengine la vijawa wake likiwa limetangulia mbele yetu. Tukafika katika nyumba moja iliyopo nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam, tukakuta walinzi wawili wakiwa wameimarisha ulinzi katika eneo hili.

“Mkuu hii ni nyumba salama. Ninainami utayapenda haya mazingira”

Mbilinyi alizungumza huku tukishuka kwenye gari zilizo ingia kwenye uzio wa nyumba hii iliyo jengwa vizuri sana japo ni ndogo kiasi. Geti likafungukwa na walinzi wawili wakatangulia mbele na tukaingia ndani ya hii nyumba.

“Waoo ni nzuri mume wangu”

Biyanka alizungumza kwa furaha huku akiendelea kutazama mazingira ya hii nyumba.

“Yaa ni nzuri mke wangu”

“Kuna baadhi ya vitu inabidi muheshimiwa tuweze kukuonyesha.”

Mlinzi mmoja alizungumza huku akichukua rimoti ndogo iliyopo mezani.

“Hii nyumba imetengenezwa kwa umaridadi wa hali ya juu. Moja hakuna risasi ambayo inaweza kuingia ndani ya hii nyumba. Kwa mfano nikiminya batani hii, sehemu zote zenye upenyo zinakuwa hivi”

Tukaanza kuona milango na madirisha ya chumba yakianza kufunga kila sehemu yenye dirisha na mlango.

“Hapa hata iweje mtu akiwa nje hawezi kuingia na wala aliyopo ndani hawezi kutoka nje”

“Wooo ni nzuri”

“Pili kuna tv yetu hapa. Unaweza kuweka upande mmoja unaonyesha tv kama kawaida na upande mwengine wa picha unaonyesha video za cctv camera. Nyuma imejitenga haina majirani, hivyo kama kuna gari au mtu ambaye atasogelea eneo hili la nyuma zaidi ya mita mia mbili, kama una angalia tv basi picha itabadilika na kuhamia kwenye video hizi za CCTV kamera na utaweza kumuona mtu huyo kama hato kuwa na madhara ya aina yoyote basi unaweza kurudisha katika eneo la kutazama tv. Na mfumo huu upo kwenye tv zote za humu ndani. Kuna tv ya chumbani, bafuni, jikoni na hapa sebleni na zote zina mfumo mmoja”

Kijana huyu alitoa maelezo ambayo kusema kweli nimeyapenda.

“Jambo jengine ambalo ni geni kwa hapa Tanzania. Tumekuwekea mfumo wa scaning pale getini endapo gari au mtu yoyote akiingia akiwa ameficha silaha ya aina yoyote kuanzia bunduki, kisu, panga hata kiwembe basi geti kuna alarm maalumu pale tumeiweka ambayo itakujulisha wewe au itafanya uweze kutambua huyo mtu ana kitu cha hatari”

“Sawa hilo nalo nime likubali”

“Pia sisi walinzi tumeweka alama za finger print ambazo system ya scaning inaweza kututambua mara tu tunapo ingia pala getini hata kama tuna silaha basi alarm inaweza kupiga.”

“Mbona sisi tulivyo ingia haikupiga alarm?”

Biyanka aliuliza huku tukimtazama kijana huyu.

“Muda ambao muna ingia nyinyi ule mfumo tuliuzima hatukuhitaji kuwafanyia suprize, tulihihitaji kutoa maelezo kwanza kisha ndio tuwaeleze”

“Ahaa hapo nime waelewa”

“Jambo jengine na la mwisho ambalo ni kubwa zaidi, hili nyumba tumeweza kuweka bunduki nne kwenye kila kona ya ukuta ulio zunguka nyumba hii. Bunduki hizi unaweza kuzi ongoza kwa simu hii popote pale utakapo kuwepo ndani ya Tanzania. Endapo mtu ataingia humu ndani ya nyumba pasipo idhni au alikuwa na lengo baya basi cha kufanya ni kuzitumia hizi bunduki kwa mfano”

Kijana huyu akaanza kuminya minya kioo cha simu hii aina ya tablet.

“Kama unavyo ona hizi bunduki zinazvyo jitokeza chini ya ardhi taratibu na tumeziwekea bomba ambalo zinaweza kupanda hadi zikapita ukuta huo na hapa unaweza kuzigeuza jinsi utakavyo. Na unaweza kuzitumia zote nne kwa wakati mmoja au moja moja kutokana na upande alipo adui yake, awe ndani ya ukuta au nje ya ukuta”

Kijana huyu alizungumza hukua kiendelea kuzizungusha zungusha bunduki hizo za kisasa ambazo hakika sijui utaalamu kama huu wameutolea wapi”

“Kila bundui moja ina mkanda wenye risasi mia tano. Kila risasi ina mm 7.92(0.312) na endapo itampiga mtu mguuni basi inaweza kumkata mtu mguu wake kama boss ulisha wahi kuona filamu ya Rambo 4 basi ile bundiki aliyo kuwa anaitumia basi inaendana na uwezo wa hizi bunduki”

“Duuuu jamani ngojeni kwanza ujuzi wote huu mumeutolea wapi?”

“Mimi nilisoma maswala ya usalama katika nchi ya Korea Kaskazini, hiyo mambo haya yote ndio wezetu wanayo yatumia kwenye nchi zao. Utakuta nyumba haina mtu ila enepo utaisogelea basi hizo risasi zake si za mchezo”

“Hapa sawa, nilikuwa nina fikiria kununua nyumba ila hii hii inatosha na muliijenga kwa muda gani?”

“Niliweza kuwapa maelezo ya kujenga nyumba hiyo kipindi tunaelekea nchini Afrika kusini na waliweza kushirikiana na kampuni moja ya wakorea Kaskazini na kazi tunashukuru Mungu kwamba imekamilika katika mufa mfupi na uimara wa hali ya juu”

Mbilinyi alijibu swala langu na kunifanya nitingishe kichwa kwa kukubaliana na kazi hii nzuri waliyo weza kuitenda.

“Nashukuru kwa juhudi zenu zote nina imani hapa nitakuwa salama”

“Tunashukuru mkurugenzi”

“Jambo jengine kesho gari lako la kutembelea tutalileta na melezo yake yote tutayatoa kesho”

“Nashukuru sana kwa kila juhudi muliyo ifanya”

“Hii nyumba ina vyumba viwili vya kulala. Hivyo karibu sana mkurugenzi”

“Nashukuru sana”

Kijana huyu akatuonyesha vyumba hivi kisha tukatoka nje na kuzunguka eneo la nyuma la hii nyumba na kukuta swimming pool, baa ndogo, gym ya kufanyia mazoezi pamoja na bustani nzuri ambayo bado maua yake hayajakua vizuri. Baada ya kuifahamu hii nyumba vizuri Mbilinyi akaomba aweze kuondoka ili aelekee kwenda kuina familia yake. Sikua na kipingamizi zaidi ya kumruhusu na wakasalia vijana wachache.

“Wasije wakawa wameweka kamera humu ndani wakawa wanatula chabo kila tunacho fanya humu chumbani”

Biyanka alizungumza huku akiangaza macho huku na kule ndani ya chumba hichi.

“Hapana bwana wange tuambia”

“Mmmm si kwa utaalamu huo walio uweka mume wangu”

Siku hii ikapita salama salmini na siku iliyo fwatia alfajiri na mapema Mbilinyi akafika nyumbani hapa huku akiwa na bahasha mkononi mwake.

“Mkurugenzi tunaweza kuzungumza?”

“Ndio”

 ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

BLOG