Search This Blog

Wednesday, November 18, 2020

SIN SEASON 2 SEHEMU YA 8/10

   


SIN SEASON 2

WRITER…………………………………………EDDAZARIA G.MSULWA
WEBSITE………………………………………… www.storyzaeddytz.com
CONTACT……………………………………….. 0657072588/0768516188
AGE……………..18+

SEHEMU YA 8 KATI YA 10


“Poa kaka, ahaa mimi nina itwa Samson nina shuhulika na maswala ya upigaji picha master wa hapa Bongo na hata nje ya Bongo. Ahaa….muonekano wako kwa kweli nime vutiwa nao, kama ina wezekana nina omba unipatie namba yako ili tuweze kuyajenga”

Evans akamtazama Samson na kutambua fika kwamba yote aliyo yazungumza ni uongo. Swali linalo mjia kichwani mwake, je Magreth ameweza kumfahamu hadi kumtuma kijana huyu kwa ajili ya kumzuga tu.

“So una hitaji namba yangu?”

“Ndio kaka, nina imani ukitokea kwenye jarida la wana mitindo una weza kuuza sana”

Evans akatabasamu, akajifikiria kwa muda kisha akaanza kumtajia Samson namba yake.

“Ina ishia na nane nane nina kuflash hapo”

Samson alizungumza ili kudhibitisha kwamba namba aliyo pewa ni ya kweli au laa. Simu ya Evans ikaita na Samson akakata simu hiyo huku akijridhisha kwamba namba aliyo pewa ni yake.

“Nashukuru sana bro”

“Usijali”

Evans akaendelea kupiga hatua kuelekea getini huku akiandika namba ya Leila kwenye simu yake na kumpihia.

“Hei ni mimi”

“Ohoo kaka mimi nimesha toka hapa nje”

“Basi nina kuja”

Evans akatoka geti kuu na kumkuta Leila akiwa ameva suruali ya jinzi iliyo mbana kisawa sawa pamoja na tisheti nyeusi.

“Nina imani wewe ni mwenyeji hapa mjini. Je ni eneo gani jengine zuri ambalo tuna weza kwenda kupata chakula cha mchana”

“Mmmm yapo mengi sana kaka yangu. Wewe niambie ni wapi twende?”

“Sema wewe kwa maana nime kuambia wewe ni mwenyeji wangu”

“Okay, tukodi bajaji au teksi?”

“Bajaji ni nzuri kwa maana nina hitaji kuuona mji wa Dar es Salaama kwa uzuri zaidi”

“Poa”

Wakaingia kwenye moja ya bajaji na kuondoka eneo hilo.

“Namba ya jamaa hii hapa”

Samson alizungumza huku akimkabidhi Magreth simu yake.

“Yaani kumbe ulikwenda kumuomba namba yule kaka!?”

Josephine aliuliza kwa mshangao mkubwa.

“Ndio kwa maana nimeona dada yangu ana teseka bure”

Magreth akainakili namba hiyo kwa uharaka huku akiwa amejawa na tabasamu usoni na akajiapiza kwamba ni lazima ampigie usiku.

“Il anime danganya mwenzenu”

“Ume danganyaje?”

Nime muambia kwamba mimi ni mpiga picha wa master wa bongo, hivyo nime penda muonekano wake nami ninge omba nizungumze naye biashara ndio aka kubali kunipatia namba. Sasa point ni kwamba je akihitaji kuona studio ita kuwaje?”

“Samson hilo lime kwisha mdogo wangu. Wewe sema vifaa vyote vinavyo hitajika kwa ajili ya hiyo studio. Nitakupatia picha, tuna funga ofisi feki na wewe uta kuwa una piga picha pamoja nami. Ni lazima nimpate yule kaka na nilazima awe wangu”

Magreth alizungumza kwa msisitizo hadi watu wote wakashangaa kwa maana kama ni kuchizika kwa mapenzi basi Magreth ame chizika kisawa sawa.

***

Raisi Mtenzi akaupitia mkataba wa raisi wa Marekeni na kundi la Bokoharamu mara ya tatu. Akamtazama mzee Mbogo pamoja na mr the Brain.

“Kweli hawa jamaa walidhamiria, hadi raisi ana saini mkataba na magaidi kwa ajili ya kumteka chief staf wangu, kweli huku walipo fika ni mbali sana”

Raisi Mtenzi alizungumza huku akiuweka mezani mkataba huo.

“Ndio hivyo muheshimiwa raisi, hawa jamaa ubabe wao ipo siku uta watokea puani”

Mr the Brain alichangia naye mada hiyo.

“Muheshimiwa raisi mimi nina ona ni heri twende mbele za sheria. Twende kwenye mahakama za kiuhalifu, nina imani lazima nchi hiyo ita adhibiwa”

Mzee Mbogo alizungumza huku akimtazama raisi Mtenzi pamoja mr the Brain.

“Hapana”

Raisi Metenzi alizungumza kisha akaka kwenye sofa lake na kukunja nne.

“Marekani ana wahisani wengi sana, ambao wengi wana mtegemea kwa mambo mengi, ikiwemo fedha, silaha na madawa. Endapo tuta hitaji kwenda kisheria basi wana weza kutuzidi kivyovyote na huu mkataba una weza ukaambiwa ni feki, na ikafikia hatua tukashindwa kesi na kujikuta tuna ingia kwenye matatizo makubwa sana ambayo pointi yao ya msingi watakayo hitaji kwenu ni sisi kuwapa hadhina ili kusamehana,huoni kwamba tuta kuwa tume poteza”

Raisi Mtenzi alizungumza huku akiwatazama washauri wkae hao.

“Hapo ume nena muheshimiwa raisi. Ila una mpango gani?”

“Nita andaa kikao cha video call na raisi wa Marekani. Nita muonyesha mkataba huo na nina imani kwamba ata shutuka sana. Nita muambia kwamba nita kwenda kuusambaza mkataba huo kwenye mitandao yakijamii na ninaimani kwamba dunia nzima ita fahamu hujuma ambazo wao ana tufanyia chini chini.”

Raisi Mtenzi akanywa maji yaliyopo kwenye glasi yake kisha akaendelea kuzungumza.

“Nina jua hato hitaji nchi yake ichafuliwe pia hato hitaji yeye kama yeye kuonekana kinyaa mbele za wana nchi wake na kama munavyo jua Wamarekani hawakopeshi kwenye maswala ya uongozi wa juu hususani uongozi wa nchi, wana weka waka mpigia kura ya kuachia madaraka na ikawa ndio mwisho wake. Hivyo nita mpa nafasi ya yeye kujikaanga mwenyewe. Nina jua wenge na bangi ambazo alikuwa ana tuwazia zita muisha”

Kila mmoja akatingisha kichwa chake.

“Muheshimiwa raisi hapo kweli ume toa pointi. Ila kuna hili jambo moja ambalo tusipo litazamia kidogo nao wana weza kulitumia kama ngao ya kujikinga na visho vyetu”

“Jambo gani mr the Brain”

“Hadi sasa hivi serikali wala si jeshi la nchi ya Nigeria walio weza kutambua kwamba ile ngome ya Bokoharamu ni nani aliye husika katika kuiteketeza. Endapo wakipenyeza siri hiyo kwa Nigeria, ina weza kutuasiri kidiplomasia.”

“Kwenye ugaidi ndugu yangu hiyo diplomasia wakitaka kuivuruga, basi nita waona ni wajinga. Miaka nenda rudi wame jaribu kuwa tekeketeza hao magaidi ila wameshindwa. Vijana wangu nane tu wame weza kumaliza mchezo. Kwanza ni lazima watushukuru kwa maana pasipo sisi, watoto wao wa kike wangeendelea kutekwa nyara na kubakwa na magaidi hao. Hivyo hata wakiataka kututaja kwa serikali ya nchi ya Nigeria kwa kweli watutaje tu na sinto ogopa chochote na wao wakileta kidomo domo, tita wachinjilia mbali”

Raisi Mtenzi alizungumza kwa kujiamini sana hadi mrs the Brain pamoja na mzee Mbogo wakajawa na mshangao mkubwa sana.

***

“Ume olewa?”

Evans alimuuliza Leila na akachia tabasamu pana sana huku akimtazama Evans kw amacho ya mitego.

“Hapana, nilikuwa na boyfriend, ila alichit na rafiki yangu hivyo nikaona nipambabe na maisha ili niweze kujitoa katika hatua moja na kwenda hatua nyingine ya kimaisha”

“Kwa hiyo kwa sasa huna boyfriend”

“Ndio sina, japo kuna wana ume wengi wana nitongoza na kunisumbua sana. Wengine wana jaribu kunihonga pesa, mali ila sibabaiki nazo kwa maana dunia ya sasa maradhi mengi.”

“Ni kweli maradhi ni mengi. Ina kupasa uwe makini”

“Kwa hilo tu usijali kaka yangu. Hivi una itwa nani?”

“Nina itwa Geogre”

“Ahaa jina zuri”

“Nashukuru”

“Je wewe ume oa?”

“Hapana”

“Ila wewe ni Mtanzania?”

“Ndio nime zaliwa hapa Tanzania n anime kulia hapa Tanzania”

“Kaka utasimama hapo mbele”

Leila alimumbia dereva bajaji na akatii amri hiyo. Wakasimama kwenye moja ya mgahawa muri ulipo eneo la Sinza. Wa kwanza kushuka ni Leila huku pochi yake akiwa ameshika vizuri, Evans akamlipa dereva huyo na kushuka kwenye bajaji. Kijana mmoja akamkwapua Leila pochi yake na kuanza kukimbia kwa kasi sana na kumfanya Leila kupiga yowe la kuibiwa. Evans hakupendezewa kabisa na kitendo hicho, akatimka mbio na kumkimbiza kijana huyo. Mafunzo aliyo yapata ya kupanda milila muku akikimbia na begi mgongoni lenye mawe ya kila hamsini hadi mia, yakamsaidia sana kumfikia kijana huyo na kumpiga mtama, ulio mnyanyua juu kimo cha mbuzi na akaanguka chini huku pochi akiiachia. Evans akaikota pochi hiyo na kumnyanyua kijana huyo kwa mkono mmoja. Sura ya kijana huyo ina onyesha bado ni mdogo sana. Evans akaona kundi kubwa la vijana likiwafwata walipo simama.

“Dogo kimbia wata kuua”

Evans alizungumza huku akilegeza mkono wake na kijana huyo akamponyoka na kumkimbia kuokoa maisha yake. Kundi hilo la watu wenye hasira kali likampita na akaanza kurudi alipo simama Leila anaye lia kwani pesa, vitambulisho na kadi zake zote za benki zipo ndani ya pochi hiyo.

“Kuwa na amani mrembo pochi yako ipo salama”

Leila macho yakamtoka huku akimtazama Evans usoni mwake. Akakabidhiwa pochi yake na kuifungua ndani na kila kitu chake akakikuta. Leila akamkumbatia Evans huku akiendelea kulia kwa furaha kwani kwenye maisha yake hajawahi kutokea mwanaume jasiri na anaye jiamini kama Georgre ambaye jina lake halisi ni Evan Shika.



“Kusema kweli hata mudi ya kuingia hapa mgahawani ime nipotea”

Leila alizungumza huku akimuachia Evans.

“So twende wapi mrembo?”

Evans alizungumza huku msisimko wa kihisia ukiwa umesha mpanda kwani joto la kukumbatiwa na Leila hakika lime amsha mambo ambayo kwa wakati huo hakuhitaji kuyaamsha.

“Mmmmm hata sielewi”

“Au twende hotelini nilipo chukua room”

“Mmmm”

“Mbona una guna?”

“Huko kweli usalama wangu uta kuwepo?”

“Kwa nini usiwepo?”

“Mmmm isije ikatoe wifi akanifumania?”

“Hahaa hapana hakuna kitu kama hicho”

“Sawa twende”

Wakakodisha bajaji na moja kwa moja ikawapeleka hadi katika hoteli ambayo Evans amechukua chumba. Evans akawasiliana na mtu wa jikoni na kumuagiza chakula walicho kihitaji, kisha akarudisha mkono wa simu hiyo sehemu alipo itoa. Macho ya Evans kila yanapo mtazama Leila hakika pepo la ngono lina mtawala kichwani mwake. Hakuna mwanaume lijari ambaye akimtazama Leila akashindwa kumtamani kabisa.

“Kwa nini sasa una ishi hapa hotelini?”

Swali la Leila likamfanya Evans kutabasamu huku akiendelea kutazama kwa kuiba mgawanyo wa mapaja yaliyo nona ya Leila.

“Nyumbani kwetu ni mkoani. Hivyo nime kuja hapa Dar es Slalaama kwa biashara zangu”

“Ahaa. Kwa hiyo wewe ni mfanya biashara?”

“Ndio”

“Una fanya biashara gani?”

“Nauza nafaka, nina toa mikoani na kuleta Dar es Salaam”

Evans aliongopea kw amaana haitahi hata judogo kuweza kugundulika au kujulikana lengo lake la kuwepo Dar es Salaam ni nini.

“Ahaa hivi kuuza nafaka ina lipa ehee?”

Kabla Evans hajajibu swali la Leila, akasikia kengele ya mlango ikigongwa. Akanyanyuka na kuusogelea mlango huo.

“Nani?”

“Chakula”

Evans akafungua mlango na kupokea sinia kubwa lililo pangwa sahani nne zenye chakula walicho kihitaji.

“Nakupatia pesa”

Evans alizungumza huku akiweka sinia hilo jui ya kitanda, akafungua wallet yake na kutoa noti tano za elfu kumi kumi na kumkabidhi muhudumu huyo.

“Nina omba na maji makubwa ila nahitaji ya moto”

“Sawa”

Evans akafunga mlango. Leila akaandaa chakula hicho na wakaanza kula huku wakiendelea na mazungumzo.

“Ehee uliniuliza kwamba biashara ya nafaka ina lipa ehee?”

“Yaa”

“Ina lip asana, kama munavyo jua jiji lenu hili watu wengi sio walimaji. Hivyo ukichukua mazoa mkoani huko na kuyaleta hapa mjini. Basi huwezi kukosa milioni mia tatu hadi mia tano, hiyo ina tegemea na mzigo ulio ununua huko mashambani na kuleta hapa mjini”

Leila akazidi kujawa na furaha kusikia kiwango hicho cha pesa kinacho tajwa. Hakika moyo wake ukaanza kujawa na tamaa ya kuzipata pesa hizo. Pasipo kujua kwamba mahesabu hayo yanayo pigwa na Evans yote ni uongo. Maji yakaletwa na muhudumu na wakamalizia chakula hicho. Evans akaanza uchokozi wa kuyatomasa mapaja ya Leila, aliye jikuta akisikilizia jinsi vidole hivyo vya Evans vikipanda taratibu kutoka kwenye mapaja hadi kifuani mwake na kuanza kuyaminya maziwa yake makubwa kiasi. Wakaanza kunyonyana denda na wakaanza kuvuana nguo na ndani ya muda mchache wakajikuta wakiwa wapo kama walivyo zaliwa na kuuanza mtanage wa kukata na shoka.

***

“Sasa Mage ndugu yangu, mwanaume ndio ume muona kwa mara ya kwanza. Una mpendaje?”

Josephine aliuliza mara tu ya kuingia ndani kwao, wakitokea Mlimani City kwenye sherehe ya Samson.

“Hilo swali ni sawa na wewe ulivyo mpenda Juma, mara ya kwanza tu ulipo muona. Japo hisia zako hukuziweka wazi kwangu, ila ukweli nilieweza kuelewa kila hali uliyo kuwa una pitia kipindi kile”

“Ila kweli, nisikulaumu sana kwa maana mapenzi ni kitu cha ajabu sana hapa duniani. Ila jambo la msingi nina kuomba uweze kuwa makini sana rafiki yangu. Si unajua wanaume hawa hawaeleweki, kama pale tu ame kutana na msichana na kuondoka naye basi ujue hajatulia”

“Uta kuta wana juana”

“Mmmm”

“Ndio uta kuta wana juana, wakaamu kuondoka kwa pamoja”

Magreth alijikuta akimtetea mwanaume huyo pasipo kufahamu kwamba ni Evans, mwanume aliye tokea kumpenda kwenye maisha yake yote.

“Haya ila tumuombe Mungu aweze kuwa ni mwanaume sahihi kwako”

Magreth akaelekea chumbani kwake, saa ya mkononi mwake ina muonyesha ni saa tatu kasoro usiku. Akaitazama namba ya George(Evans) kwa sekunde kadhaa, kisha akaipiga huku mapigo yake ya moyo yakimuenda kasi sana. Kwa bahati mbaya akakuta namba hiyo haipatikani hewani.

“Akkghaa…..”

Magreth alilalama huku akirudia kuipiga ila majibu aliyo kutana nayo ni yale yake kwamba namba hiyo haipatikani hewani.

‘Au katoa namba ya gari huyu?’

Magreth aliwaza kichwani mwake na kukosa jibu la uhakika.

***

“Baby, ume nitomb** vizuri”

Leila alizungumza huku akiwa amejalaza kifuani mwa Evans.

“Kweli?”

“Haki ya Mungu vile. Toka niyajue mapenzi, sijawahi kukojoleshwa. Ila leo ume nikojolesha kwa mara ya kwanza”

“Nina shukuru kwa hilo. Una ishi wapi hapa Dar es Salaam?”

“Nina ishi magomeni”

“Ahaa sawa sawa, uba boy friend?”

“Hapana”

“Acha kunitania, uzuri wote huo?”

“Haki ya Mungu vile sina mwanaume. Japo wanaume wengi wame kuwa wakinitongoza ila nina wakatalia”

“Ahaa so magomeni una ishi peke yako?”

“Nina mdogo wangu wa kike ndio nina ishi naye”

“Okay so muna nyumba nzima?”

“Hapana, nime panga chumba na sebule”

“Kazi yako ina kulipa?”

“Hivyo hivyo Mungu ana bariki chochote kina kwenda kinywani”

“Ohoo sawa. Sasa kuna kazi moja nina hitaji kukupatia”

“Kazi gani baby”

“Nita kuambia asubuhi sasa hivi nipatie kitu rogo ina penda”

Evans alizungumza kisha akayanyuka na kuyapanua mapaja ya Leila na kuanza kumnyonya kitumbua chake taratibu na wakaendelea na mtanange wao wa kukata na shoka. Kila mtu alijikuta akifurahia tendo hilo hadi Leila akanza kumuomba Evans aweze kumuoa.

Hadi asubuhi kuna pambazuka kila mmoja kila mmoja mwili wake alihisi ukiwa umeisha nguvu. Evans akashuka kitandani taratibu na kuanza kufanya mazoezi mepesi mepesi ya viungo ikiwemo push up. Misuli ya Evans iliyo jengenga vizuri mwilini mwake, hakika ikamfanya Leila azidi kumpenda Evans, japo ni masaa machache sana wame weza kuyatumi wakiwa pamoja ila amejikuta akimpa Evans moyo wake wote.

“Ume amka?”

Evans alizungumza huku akwia amepiga msamba huku akiwa ametunisha misuli yake.

“Yes baby, kumbe wewe ni mtu wa mazoezi ehee?”

“Yaa kidogo tu. Njoo tufanye?”

“Mmmm hapana mpenzi wangu kwa maana si kwa kunisugua kule usiku. Yaani hapa miguu yangu haina nguvu kabisa”

“Pole mpenzi wangu”

“Nashukuru, ehee niambie ni kazi gani ambayo una hitaji kunipatia?”

“Niambie pale una lipwa kiasi gani?”

“Laki nne kwa mwenzi”

“Ohoo sawa. Sasa nahitaji ufanye jambo moja kuna mtu nina hitaji umfwatilie na unipatie data zzake nita kulipa kiasi chochote utakacho kihitaji”

“Mmmm una niogopesha mpenzi wangu. Huyo mtu ni nani?”

“Ni mtumishi mmoja ana itwa nabii Sanga”

“Huyu ambaye ana kanisa lake kubwa hapa…..”

“Yaa huyo huyo.”

“Mmmm sasa mume wangu mtu huyo ni mkubwa sana hapa nchini na mbaya zaidi mwanaye ame olewa na mtoto wa raisi. Sasa ita kuwaje?”

“Nina kupa mbinu ya kufanya. Nina imani tukikamilisha mpango huu kila jambo lita kuwa sawa”

Evans akaanza kumuelezea Leila ni kitu gani wana paswa kukifanya.

“Nita weza kuifanya hiyo kazi japo ni hatari?”

“Usijali mpenzi wangu endapo tukifwata utaratibu kila jambo lita kwenda sawa”

“Poa”

Evans akafungua begi lake na kumpatia Leila dola elfu moja kwa ajili ya kuainza kazi hiyo ambayo ana amini kwa kupitia Leila basi ana wez akupata taariza za nabii Sanga. Baada ya Leila kuondoka, Evans akawasha simu yake na kukuta jumbe za meseji kwamba kuna namba ambayo machoni mwake ni ngeni ime mpigia. Kabla hajaikagua vizuri simu yake ikaanza kuita.

***

Magreth kitu cha kwanza baada ya kuamka, akaishika simu yake. Akaitazama namba aliyo pewa na Samson, akashusha pumzi nyingi kisha akapiga, simu ikaanza kuita na akajikuta akikurupuka kwa haraka sana na kukaa kitako kitandani huku akimeza mafumba ya mate kwa maana hajui ni nini kinacho kwenda kuzungumzwa. Simu hiyo ika pokelewa naukimya ukatawala. Magreth akatamani kuzungumza jambo ila akajikuta akishikwa kwa kigugumizi.

“Nani?”

Sauti nzito ya kime ukamchanganya sana Mageth na mwili mzima uka sisimka kimahaba.

“Aha….a…”

Magreth akajitahidi kuzungumza ila kigugumizi kilicho mkamata akashindwa kabisa kujibu alicho ulizwa. Mlango ukafunguliwa na Josephine akaingia huku akiwa amejifunga kanga moja. Josephine akaka pembeni ya Magreth na kkumtazama jinsi anavyo babaika. Simu ikakatwa na kumfanya Magreth kushusha pumzi nyingi sana huku akimtazama rafiki yake.

“Una nini?”

“Nime mpigia yule kaka. Kusema kweli nime shindwa kuzungumza.”

“Weee yaani na ujanja wote huo ume shindwa kuzungumza naye?”

“Ndio yaani nimejikuta nikishikwana kigugumizi cha ajabu”

“Mmmm”

“Haki ya Mungu vile”

“Sasa ita kuwaje kama una shindwa kuzungumza”

“Una jua mwanamke kumtongoza mwanaume ni shida”

“Yaa ni shida, ila nipe simu”

“Una taka kufanyaje?”

“Kukusaidia”

Magreth akamtazama Josephine kwa sekunde kadha akisha akamkabidhi simu yake. Josephine akaipiga namba hiyo na kuweka loud speaker. Simu ika pokelewa.

“Nani wewe, mbona una piga simu na kukaa kimya?”

Evans alizungumza kwa sauti ya nzito na ya kukwaruza ambayo si Magreth wala Josephine aliye weza kuitambua.

“Ahaa samahani kaka yangu”

“Bila samahani, nani wewe?”

“Nina itwa Jose au Josephine”

“Una taka nini?”

“Jana mchana pale mlimani City niliweza kukuona na mdogo wangu alikuomba namba ya simu akikueleza kuhusiana na maswala ya kupiga picha za wana mitindo.”

“Yaan ime kumbuka. Mbona haja nipigia yeye?”

“Ahaa mimi ndio meneja masoko. Hivyo kama huto jali kaka yangu nina kuomba tuonane pale pale Samaki Samaki”

“Kwa kuonana pale ita kuwa ngumu. Niambie ofisini zenu zipo wapi ili nije?”

Josephine akamtazama Josephine kwa maana hadi sasa hawana ofisini na hiyo kazi wanayo izungumzia ni uongo.

“Ahaa kwa sasa nipo nje ya ofisini. Kama huto jali tukutane sehemu tofauti na ofisini”

“Poa basi tukutane Sinza, kwenye mgahawa mmoja una itwa AJ.”

“Poa nashukuru”

“Baada ya dakika kumi nita kuwepo hapo”

“Sawa nita fika hapo baada ya nusu saa”

Josephine mara baada yakukata simu wakakumbatiana na Josephine huku wakiwa wamejawa na furaha kubwa sana kwani leo rafiki yake ana kwenda kukutana na mwanaume ambaye ame mchanganya kimapenzi.



“Nusu saa kutoka huku kigamboni hadi Sinza halitoshi kama tukitumia gari. Cha kufanya tutumie pikipiki”

Magreth alishauri na kwa haraka wakaanza kujiandaa na kisha wakaondoka nyumbani hapo. Kwa ujuzi wa Magreth na uwezo wake wa kuendesha pikipiki hiyo, wakafanikiwa kufika Sinza katika mgahawa walio elekezwa ndani ya muda mchache tofauti na vile walivyo weza kumuahidi Evans. Wakaingia kwenye mgahawa huo ambao kidogo ume jaa watu. Wakaangaza angaza na Evans akaonyoosha mkonono kuwaashiria kwamba wamuone.

“Yule pale”

Magreth alizungumza huku akiwa amejawa na furaha sana. Mapigo yake ya moyo yakamuanza kumuenda kasi huku hali tofauti ikimtawala mwili wake. Evans akasimama na wakaanza kusalimiana.

“Mimi nina itwa Josephine ndio tulizungumza kwenye simu n a huyu hapa ni rafiki yangu ana itwa Magreth”

Josephine alizungumza huku uso wake ukiwa ume jawa na tabasamu pana. Bumbuwazi lililo mkamata Magreth hakika likamfanya hadi Evans kuhisi kama ame fahamika kwa maana msichana huyo ana mfahamu vizuri sana.

“Mage”

Josephine alimgonga kidogo Magreth begani mwake, kwani Evans amenyoosha mkono kwa sekunde kadhaa pasipo Magreth kuupokea.

“Yeah habari”

Magreth alizungumza huku akishusha pumzi.

“Salama, nina itwa George. George Sanga”

Evans alizungumz akwa suati nzito ambayo ikazidi kumchanganya Magreth.

“Tuna shukuru kukufahamu”

Magreth alijibu huku wakiachiana mikono na Evans wanaye mfahamu kwa jina la George.

‘Kweli Mungu ana nipenda, yaani maandui zangu wamajileta wao wenyewe na mbaya hawajanifahamu’

Evans alizungumza kimoyo moyo huku akimtazama Magreth aliye jikuta akihisi aibu kwa kukodolewa macho hivyo na kujikuta akitazama chini.

Ehee niambieni, lengo la kuonana na mimi ni nini?”

Evans aliendelea kuzungumza kwa sauti ya kunguruma huku akimtazama Josephine.

“Ahaa…a.a..aaa”

Josephine naye alijikuta akijing’ata ng’ata kwa maana katika maisha yake siku zote huwa ana ogopa sana kuongopea.

“Vipi?”

“Ahaa kusema kweli ni jambo moja kaka yangu George. Nime tokea kukupenda sana, toka nilipo kuona pale jana Samaki Samaki, hakika ume weza kuuteka moyo wangu. Hapa nilipo nina jihisi mwili wangu kuishiwa nguvu kwa upendo wako”

Magreth alizungumz akwa kujiamini hadi Josephine macho yakamtoka kwa maana hakutajarijia kama Josephine ana weza kufunguka kwa namna hiyo. Evans akatabasamu huku akimtazama Magreth usoni mwake, muhudumu akafika mezani hapo.

“Wasikilize wageni wangu”

“Muna tumia nini dada zangu”

“Mimi nina omba Safari ya baridi”

Magreth alizungumza kwa kujikaza.

“Safari!!?”

Josephine aliuliza kwa mshangao kwa maana toka amfahamu Josephine hajawahi kumuona siku hata moja akiwa ana kunywa kilevi chochote. Evans naye macho yakamtoka kwa maana na mtambua vizuri Josephine na kuhitaji kunywa huko pombe kuna kitu kinacho endelea kwenye kichwa chake.

“Nisikilize dada, tuletee Cocacola mbili, hiyo safari achana nayo”

“Hapana Josephine nina hitaji kunywa?”

“Hapana, ingekuwa tume kuja na gari hapo sawa ninge kuruhusu kunywa. Ila tumekuja na ile tukutuku, mimi siwezi kuiendesha bwana”

Josephine alionyesha wasiwasi wake upo wapi.

“Mletee Cocacola”

Evans alimbidi kuingilia kati jambo hilo.

“Sawa, je muna tumia chakula gani?”

“Tuta kuambia tukuhitaji”

Josephine alijibu na muhudumu huyo akaondoka na baada ya muda akarudi akiwa na chupa mbili za Cocacola pamoja na glasi mbili zenye tishu ndani. Baada ya muhudumu kuondoka maongezi yakaendelea.

“Ume niambia una nipenda kwa namna gani?”

Evans akajifanya kama vile haijui kitu alicho ambiwa kina maanisha nini.

“George nina imani kwamba uta kuwa una nishangaa sana. Ila mimi sio wale wanawake malaya, mimi nime zungumza kitu kilichopo moyoni mwangu. Nina kupenda sana George, nilisha wahi kumpenda mwanaume kama hivyo, ila Mungu hakupenda niwe naye hivyo tuliachana. Ila wewe toka nilipo kuona, moyo wangu uliweza kustuka sana, tafadhali Geogre naomba unielewe”

Maneno ya Magreth yakamfanya Josephine kufumba macho yake kwa maana badala ya rafiki yake kutongoza sasa ni wakati wa yeye kutongoza na jambo hilo ni aibu kubwa sana kwa wanawake wengi wa Kitanzania.

“Una jua mimi siwajui nyinyi ni kina nani, muna jishuhulisha na nini. Niliwaona tu jana pale mgahawani, sasa ukiniambia hayo maneno nina weza kupata mashaka. Isije mukawa ni watu mulio tumwa na watu wasio kulikana na mukaniteka”

“Hahaaa hapana kaka yangu. Mimi ni chief staff ikulu”

Josephine alizungumza hukua akichomoa kitambulisho chake kwenye pochi na kumpatia Evans, aliye kisoma kwa sekunde kadhaa.

“Waoo hongera sana. Kumbe nipo na mshauri mkuu wa raisi hapa?”

“Ndio, huyu rafiki yangu ana husika kwenye maswala ya usalama zaidi”

“Una taka kuniambia Magreth ni usalama wa taifa?”

“Hapana, kwa maana hana kitambulisho hicho. Ila ana dili sana na mambo ya kiusalama. Endapo huko mbele tukizidi kuwa marafiki uta zidi kumfahamu vizuri”

Macho ya Magreth hayakusita kutazama macho ya Evans na kujikuta akianza kuyafananisha macho hayo na macho ya mpenzi wake Evans.

“Magreth”

Evans aliita.

“Beee”

“Huyo mpenzi wako, ilikuwaje ukaachna naye?”

“Ni story ndefu sana, ila nikiwa vizuri siku nita kusimulia mambo yote yalivyo kuwa”

“Mmmm sawa, hakuna shaka. Kutokana mimi nina kaa hoteli kwa sasa kwa maana nime kuja hapa Dar kwa mambo ya kibiashara, nita tafuta siku ya kukaa na wewe, tuzungumze mambo mengi sana”

Simu ya Evans ikaanza kuita, akaitazama kwa sekunde kadhaa na kukuta ni Leila.

“Samahani jamani”

Evans alizungumza huku akisogeza kiti nyuma na kusimama, akatoka nje ya mgahawa huo na kuipokea simu hiyo.

“Mage aisee ume jikaza kwa kweli”

“Yaani wee acha, sijui hata ujasiri niliutolea wapi”

“Una jua hadi nilihisi tumbo lilikuwa lina niuma, ulipo kuwa una zungumza yale maneno”

“Kupenda kubaya rafiki yangu, yaani huyu kaka amenichanganya kwa kweli. Alafu nime gundua jambo moja kwake”

“Jambo gani?”

“George ana macho kama ya Evans. Yaani hayana utofauti kabisa, kilicho na utofauti ni sura zao”

“Ndio ujitahidi kutulia naya rafiki yangu. Si una jua wanaume jinsi walivyo, huyu ukimletea itikadi za kina nabii Sanga ita kula kwako”

“Yaani we acha akinikubalia, haki ya Mungu nina mbebea ujauzito”

“Ohoo!!”

“Haki ya Mungu vile, lazima nimbebee ujauzito”

“Kazi kweli kweli”

Josephine alizungumza huku akimtazama Evans aliye simama nje akiendelea kuzungumza na simu hiyo.

“Hakikisha una kuwa makini”

“Usijali mume wangu, jioni si tuna weza kuonana kwa maana nikirudi kutoka kwa rafiki yangu, nita kuandalia chakula kizuri sana”

“Usijali, tuta wasiliana”

“Nashukuru kwa wito wako. Nina kupenda pia?”

“Nami pia nina kupenda”

“Haya lunch njema”

“Asante”

Evans akakata simu na kuirudisha mfukoni mwake. Akarudi ndani na kukaa kwenye kiti chake.

“Jamani munaonaje tukaagiza chakula”

“Ni kweli”

Josephine aliunga mkono. Evans akamuita muhudumu na wakaagiza chakula kisha wakaanza kula taratibu, huku kwa mara kadhaa Evans na Magreth wanayagonganisha macho yao na kujikuta wakitabasamu. Kumbukumbu za Evans zikaanza kurudi nyuma kama mkanda wa video. Akakumbuka kichochoro alicho mkuta Magreth akiwa ana sumbuliwa na vibaka huku akiwa ameshika deli lililo jaa maandazi mkononi mwake. Akakumbuka jinsi alivyo anza kupambana na wahuni hao, hadi ikapeleka kuchomwa kisu.

Akakumbuka kipindi walipo kuwa wakishirikiana kuuza mgahawa na Magreth huku akiamini kwamba ndio mpenzi wa maisha yake yote, ila mambo yakabadilika mara baada ya kumjua nabii Sanga kwa upande wa pili ambao ndio wa chui, kwani laiti inge kuwa sio Magreth basi ile siku waliyo kutwa kitandani basi risasi ambayo inge toka kwenye bastola ya nabii Sanga inge kuwa halali yake.

***

Leila moja kwa moja akaelekea kwa rafiki yake Caro, mara baada ya kupewa ruhusa ya kwenda huko na Evans. Umbea ambao rafiki yake Caro alimueleza kwamba ana hitaji kumuambia akifika tu nyumbani kwake, hakika ume mfanya ajitahidi kuwahi nyumbani hapo. Akaribishwa vizuri na Caro na wakakaa sebleni

“Ehee rafiki yangu, mbona ume rudi haraka haraka”

“Yaani wee acha tu shosti yangu. Katika safari zangu zote nilizo wahi kutoka nje ya nchi hii safari ya wakati huu ilikuwa na mikosi pia ikawa na baraka kubwa”

“Ehee nipe mchapo shosti yangu. Ila ngoja kwanza, shemeji yupo?”

“Mmmm shemeji yako ame toka, amekwenda kutazama zake mpira. Ana sema sijui Manchester inacheza huko, hivyo ame toka juu juu”

“Hapo sawa kwa maana nisije nika teleza hapa mambo yakawa sio mambo bure”

“Yaa ni kweli. Acha sasa niendelee”

“Ehee niambie”

Leila alizungumza huku akikunja nne kabisa, ili kusika umbea huo.

“Bwana si tuliondoka hapa Tanzania kwa ndege ya Fly Emirates?”

“Ndio nakumbuka siku ile ulipo toka kukata tiketi ulipita pale kazini kwangu”

“Ewalaa. Ebwana, safari ilipo anza si ndege ikapata ajali”

“Weeee!!?”

Leila alishangaa sana.

“Ndio, ila cha kumshukuru Mungu iliangukia ziwani na watu wote tuka toka salama”

“Ehee ikawaje sasa?”

“Tukasafirishwa na ndege za kijeshi hadi katika kiwanja cha Congo kusubiria hali ya hewa ikae vizuri. Sasa tukiwa pale uwanjani, si nikakutana na nabii Sanga”

Leila akastuka kidogo ila akazuia mstuko wake.

“Ehee?”

“Bwana nikaanza kuzungumza naye. Nashukuru Mungu hakuwa na mke wake wale walinzi wake. Tukaanza kuzoeana na tukaenda Nigeria pamoja. Yaani nika sema hii ndio nafasi simuachii yule mzee kwa maana ana pesa ya kufa mtu”

“Kama kawaida yako?”

“Yaani, sikujali ni mtumishi wa Mungu au nani, yaani nilicho kifanya ni kumtega hadi akaingia laini. Mtoto nilimpa mauno yule mzee, yaani nikaenda mbali hadi nikampa mkund***”

“Weee acha utani?”

“Haki ya Mungu vile. Mzee kamla bata wangu”

“Hakuanza kukuombea kama una mapepo?”

“Nyoo aanzie wapi kwa mfano. Ila mzee kumbe naye yupo vizuri bwana, damu bado ina mchemka, yaani alinila bata hadi nikaanza kuomba poo mimi. Ila shosti yangu ni siri haya ninayo kuambia”

“Wala usijali, mimi na wewe damu damu, siri yako siri yangu, yangu ya kwako”

“Ni hapo tu ninapo kupendea shosti yangu. Yaani mzee alinipa dola elfu hamsini, sawa na milioni mia na usheee”

“Wacha wee”

“Yaani nikanunua bidhaa zangu baada ya hapo nikarudi naye, ndege kanilipia. Hapa nilipo yaani nasubiria simu yake. Yaani akiniita mafichoni basi nita hakikisha nina kwenda kumpa show za kizaramo hadi yeye mwenyewe aninunulie nyumba au kunijengea”

“Ila kuwa makini, si una jua ana mke na mtoto wake yule aliye olewa na mtoto wa raisi?”

“Nalijua hilo shosti yangu”

“Basi usije uka jikuta una tekwa na watu wasio julikana. Ita kula kwako”

“Usijali rafiki yangu, nipo makoni tena sana. Ila mchele ndio huo shosti yangu. Yaani nilijitahidi kuubania moyoni mwangu, ila nimeshindwa kabisa nime ona nikuambie ndugu yangu”

‘Laiti unge jua ninacho muwazia huyo nabii Sanga wala usinge zungumza hivyo Caro rafiki yangu’

Leila alizungumza kimoyo moyo huku akimtazama Caro aliye jawa na furaha kubwa sana.

“Pia kuwa makini shemeji asijue?”

“Hawezi kujua, si unajua hapa mimi ndio mume, yaani huyu nikimpa pesa tu hata kama ana hasira basi zina mnyeyu…….”

Caro akajikuta akikatisha sentensi yake huku akitazama namba ngeni iliyo ingia kwenye simu yake. Akaipokea na kuiweka simu sikioni mwake.

“Ni mimi upo wapi?”

Sauti ya nabii Sanga ilisikika na kumfanya Caro kujawa na tabasamu pana sana usoni mwake kiasi cha kumfanya Leila kumshangaa kwa maana hatambui ni kwa nini simu huyo aliyo pigiwa ime mfurahisha kiasi hicho.



“Yes baby”

Caro alizingungumza kwa sauti ya kimahaba na kumfanya Leila moja kwa moja atambue kwamba huyo anaye ambiwa hivyo ni nabii Sanga.

“Upo wapi?”

“Nipo home”

“Nina hamu na wewe”

“Waoo hata mimi nin hamu na wewe”

“Jiandae alafu baada ya robo saa nita kuambia ni wapi uweze kunifwata”

“Sawa mpenzi wangu nina kupenda sana”

“Nashukuru”

Simu ikakatwana kumfanya Caro kuruka kwa furaha.

“Shosti vipi?”

“Yaani huyu mzee hato kufa haraka, yaani tume toka kumtaja sasa hivi na amepiga simu”

“Weee”

“Haki ya Mungu ameniambie nijiandae baada ya robo saa ata nipia. Ndugu yangu acha nijiandae basi haraka haraka, hapa asije akapiga simu nikajikuta bado sijajiandaa. Mtu mwenyewe ana onekana ana penda sana kwenda na muda”

“Sawa shosti yangu, acha basi mimi niondoke”

“Ngoja kwanza nioge kuna zawadi zako nilikuchukulia. Nakuletea sasa hivi”

Caro akaiweka simu yake juu ya meza na kuelekea chumbani kwake. Kwa haraka sana Leila akaichukua, na kuitazama namba hiyo iliyo piga, akaikremisha kwa uharaka sana kichwani mwake kisha akairudisha simu ya Caro sehemu alipo iweka. Baada ya dakika mbili Caro akarudi akiwa ameshika mfuko mkubwa.

“Shosti yangu, nime kununulia gauni, viatu chani na hereni vipo katika mfuko huo”

“Waooo asante sana rafiki yangu, yaani sijui nikulipe nini?”

“Usijali ndugu yangu wewe ni rafiki yangu. Hizo herein na cheni zote ni pure gold”

“Woooo jamania Caro, vyote hivi ni vyangu?”

Leila alizungumza huku akiwa amejawa na mshangao mkubwa sana.

“Yeah vyote ni vyako, huniamini?”

“Nina kuamini, asante sana rafiki yangu”

“Usijali. Mimi na wewe ni ndugu, tume saidiana kwenye mambo mengi sana, hukuniacha nikiwa kwenye shida na hata kwenye huzuni ume kuwa pamoja nami. Nakupenda sana rafiki yangu”

Caro alizungumza kwa hisia kali sana na upendo wake kwa rafiki yake una tokea moyoni mwake.

“Nakupenda sana rafiki yangu”

Wakakumbatiana kwa furaha sana, kisha taratibu wakaachiana.

“Acha mimi nioge, nita kupitisha hadi kituoni upande bajaji nami nita elekea huko alipo niita Sanga”

“Hakuna shaka rafiki yangu”

Caro akarudi ndani kwake na kumuacha Leila akianza kukagua zawadi hizo. Hakika rafiki yake ame weza kumletea gauni ambalo siku zote alikuwa ana liona kwenye mtandao na kulipenda.

‘Caro nakupenda sana rafiki yangu. Ila huyu mtu uliye naye ndio utajiri wangu’

Leila alizungumza kimoyo moyo. Baada ya dakika kumi Caro akatoka sebleni huku akiwa amejiandaa tayari kwa safari hiyo. Hazikuisha hata dakika tatu, simu ya Caro ikaanza kuita na akaipokea kwa haraka.

“Yes”

Caro alizungumza huku akiwa na tabasamu pana usoni mwake. Nabii Sanga akamueleza ni sehemu gani amfwate na kumsisitizia aje peke yake.

“Nusu saa nita kuwa nime fika hapo mpenzi wangu”

Caro alizungumza kimahaba kisha akakata simu.

“Shosti mambo yame kwiva. Tuondoke”

Wakatoka nje na kuingia ndani ya gari na taratibu wakaondoka eneo hilo. Leila akashuka kwenye kituo cha waendesha bajaji na pikipiki na Caro akaendelea na safari zake. Leila akapanda pikikipi na kuelekea nyumbani kwake.

***

“Naombeni kuondoka”

Evans alizungumza huku akionekana kuwa na hasira kidogo. Kumbukumbu za matukio mabaya aliyo fanyiwa nyuma na nabii Sanga, pamoja na Magreth yakauchafua moyo wake.

“Mbona haraka na una onekana una hasira”

Josephine alizungumza huku akimtazama Evans usoni mwake.

“Kuna watu nina hitaji kuonana nao. Kidogo wame nichanganya kwenye biashara zangu, hivyo nina waomba niweze kuondoka”

“Geogre”

Magreth aliita kwa sauti ya upole.

“Naam”

“Kama sisi ndio tume kuudhi tafadhali, tuna kuomba uweze kutusamehe”

“Hapana, ile simu niliyo toka kuipokea nje ndio ime nikasirisha”

Evans aliongopea ila ukweli kila anapo mtazama Magreth ana kumbuka safari yake ya mateso makubwa makubwa ilianzia kwake. Moja ikiwa ni kuchomwa kisu na vibaka, mbili kuumizwa moyo wake isitoshe akapokonywa msichana huyo na mzee ambaye alikuwa akimumini kama mtu mzuri sana kama anavyo onekana mbele ya macho ya watu wengi ndani ya nchi ya Tanzania na nje ya nchi ya Tanzania. Akakumbuka jinsi alivyo mpata Julieth ambaye yeye ndio nusu apoteze uhai wake, kwani watu walio mteka hakika walihitaji kuinyofoa roho yake. Ila Mungu tu ndie aliye msaidia hadi akapata msaada kutoka kwa mzee Msese, mganga anaye ishi milimani sana katika mkoa wa Morogoro.

“Geogre, Geogre”

Magreth aliita huku akimtazama Evans aliye shikwa na bumbuwazi.

“George”

Magreth ilibidi amuite huku akimtingisha mkono wake na kumfanya astuke.

“Yes”

“Upo sawa baba?”

“Ndio, ndio”

Evans alizungumza huku macho yakimpepesuka. Akanyoosha mkono wa kulia juu na muhudumu aliye muhudumia akafika.

“Naomba bili ya meza nzima”

“Sawa”

Muhudumu akaondoka na baada ya dakika mbili akarudi akiwa na kijitabu ambacho ndani kina risisti ya kila kitu alicho kitumia. Evans akafungua kitabu hicho na kusoma kiasi anacho daiwa, akatoa kiwango hicho na kukiweka ndani ya kitabu hicho na kumrudishia muhudumu.

“Nashukuru sana”

Muhudumu alizungumza kwa sauti ya ukarimu.

“Kuna munacho kihitaji cha zaidi?”

Evans aliwauliza huku akiwatazama Magreth na Josephine kwenye nyuso zao.

“Hapana asante kwa lunch”

Josephine alijibu.

“Sawa dada una weza kwenda”

Evans akamuruhusu muhudumu kuondoka.

“Ni lini tuna weza kukualika nyumbani kwetu ukaja kula nasi japo chakula cha usiku”

“Kutokana muna namba yangu na nina namba ya Josephine hapa basi nita wasiliana nanyi pale nikiwa na muda. Asanteni kwa kuonana na mimi mchana mwema”

Evans alizungumza huku akisimama, Magreth na Josephine nao wakasimama, wakapena mikono, ila Magreth akaona hawezi kumucha Evans kuondoka pasipo kumkumbatia. Akamkumbatia kwa nguvu kwa sekunde kumi na kumuachia huku akihisi hamu ya kufanya tendo la ndoa ikimpanda kwa kiwango kikubwa sana.

“Mchana mwema”

Evans mara baada ya kuzungumza hivyo akaondoka kwenye mgahawa huo na kumuacha Magreth akiwa ameshikwa na bumbuwazi kubwa.

“Mage”

“Ehee?”

“Mbona ume kodoa tu macho?”

“Yaani nilivyo mkumbatia George nime jikuta nikishikwa na nyege yaani hapa nilipo huku chini pamesha lowana kwa maji”

“Weee”

“Haki ya Mungu vile”

“So utafanyaje?”

“Turudi tu nyumbaani”

“Kwa hali hiyo kweli uta weza kuendesha pikipiki”

“Nita jitahidi”

Magreth na Josephine wakaondoka eneo hilo, wakapanda kwenye pikilipi yao na kuondoka eneo hilo.

***

Caro akasimamisha gari lake kwenye mtaa ambao una nyumba zilizo jipanga vizuri huku kila nyumba ikiwa na geti kubwa. Kwa haraka haraka mtaa huo wana ishi matajiri. Akatoa simu yake na kuipiga namba ya nabii Sanga.

“Nime fika kwenye huu mtaa.”

“Kuna nyumba ina geti jeusi, na namba ya nyumba ni mia tatu na mbili KL Ipo upande wa kushoto, ukifika hapo moja kwa moja simama geti lita funguka. Upo kwa miguu au gari?”

“Nipo na gari langu”

“Sawa lita funguka”

Caro akakata simu na kuanza kuendesha gari lake taratibu taratibu hadi kwenye nyumba hiyo ambayo ina gorofa moja. Taratibu akasimamisha gari lake nje ya geti hilo lililo anza kufunguka taratibu, Caro akajaribu kuangaza kama kuna mlinzi anaye fungua geti hilo, ila kagundua kwamba geti hilo lina funguliwa kwa umeme. Akasimamisha gari lake nyuma ya gari lililopo eneo hilo. Akashuka na kushuhudia geti hilo likijifunga. Akaanza kutembea kuelekea ndani na akagonga mlango wa mbele, mlango uka funguka wenyewe pasipo kufunguliwa na mtu. Akamkuta nabii Sanga akiwa amekaa sebleni huku amevalia bukta na tisheti nyepesi.

“Karibu sana mpenzi”

Nabii Sanga alizungumza huku akiweka glasi yake ya wyne mezani, wakakumbatiana na Caro kisha wakaanza kunyonyana denda.

“Karibu sana kwangu”

“Hapa ni kwako pia?”

“Yes, ila hii ni nyumba yangu ya siri ambayo mara nyingi huwa nikiwa nina mawazo yangu binafsi basi nina kuja kukaa hapa.”

“Mke wako hapafahamu?”

“Hajui, nime sema ni nyumba yangu ya siri ambayo wewe ndio mtu wa kwanza kuitambua na sinto pesa siku hata mmoja umueleze mtu kwamba hapa ni kwangu”

“Usijali mpenzi wangu, siwezi kuzungumza hivyo”

“Vipi nikumimi nie wyne?”

“Yes nimiminie”

Nabii Sanga akaelekea jikoni na kumuacha Caro akishangaa shangaa uzuri wa nyumba hii.

‘Haki ya Munu wantu wana pesa yaani hii ni nyumba ya kupumzikia tu’

Caro alizungumza kimoyo huku akiendelea kushangaa shangaa eneo hilo. Nabii Sanga akarudi akiwa ameshika glasi, akamimina kiasi cha wyne na kumkabidhi Caro. Taratibu wakaanza kunywa huku nabii Sanga akiendelea kumchunguza Caro kwa macho yaliyo jaa umakini.

“Beb mbona una nitazama sana?”

Caro alizungumza kwa sauti ya kudeka na kumfanya nabii Sanga kutabasamu.

“Nime kuita hapa kwa ajili nina hitaji kukupatia kazi”

“Kazi gani baby”

“Kuna wasichana wawili ambao nina hitaji uwe na ukaribu nao sana. Mmoja ana fanya kazi ikulu na mwengine ana isaidia serikali. Wasichana hao ni hatari sana kwa sababu huyu mmoja anaye fanya kazi ikulu ana uwezo wa kuweza kuona mambo yajayo. Huyu wa pilia naye isaidia serikali ana uwezo mkubwa sana wa kupigana.”

“Mmmm baby so una watakia nini?”

“Ninacho hitaji wewe kukifanya ni kuwa marafiki zao. Hakikisha wana kuamini sana na uta kuwa una nipa kila aina ya habari walio nayo”

“Wapo hapa hapa Dar na wana ishi Kigamboni”

“Majina yao ni nani na nani?”

Nabii Sanga akatoa simu yake mfukoni na kuwaonyesha picha ya Magreth na Josephine.

“Mmmm mbona hawa ni rafiki zangu. Si wana sali kanisani kwako?”

“Ewalaaa, walikuwa wana sali kanisani kwangu, japo sasa hivi sitambua wana sali wapi”

“Sawa mpenzi wangu, nita kusaidia na nita jaribu kutafuta namba zao za simu kisha nita rudisha mazoea nao”

“Nashukuru kwa hilo, njoo hapa”

Nabii Sanga alizungumza kwa furaha na taratibu Caro akamkalia mapajani mwake na wakaanza kutomasana na wote wakajikuta wakiziweka glasi zao mezani na kuendelea na mitomasano hiyo iliyo wapelekea wote kujikuta wakivua nguo moja baada ya nyingine.

***

“Vipi mapumziko yenu yamekwendaje?”

Raisi Mtenzi alimuuliza Julieth na Jery mara baada ya kurudi kutoka kwenye mapumziko visiwani Zanzibar.

“Kwa kweli tuna shukuru sana baba hapa akili zetu zime kaa vizuri kabisa. Nime pata muda wa kutosha wa kukaa na mume wangu na kufurahia maisha”

“Ni jambo zuri sana, hivyo ndivyo inavyo paswa. Hata kipindi cha ujana wangu, nilitumia muda mwengi sana na mama yenu.”

Raisi Mtenzi alizungumza kwa sauti ya upole sana.

“Ahaa baba vipi kuna mpya gani?”

Jery aliamua kuzugisha mazungumzo hayo kwa maana haitaji baba yake akumbukie maisha aliyo ishi na mama yake.

“Mpya hakuna, zaidi ya kwamba tuna pambana katika kuijenga nchi hususani jiji hili”

Simu ya Jery ikaingia meseji, akaitoa mfukoni na kuifungua na kukuta ni namba ya Shani.

‘Nipigie nina habari muhimu’

Jery mara baada ya kuisoma meseji hiyo akaifuta na kuirudisha simu mfukoni mwake.

“Baby kuna ile zawadi ya baba ipo wapi?”

Julieth aliuliza huku akimtazama Jery.

“Kuna begi nahisi tume sahau kwenye gari ngoja nikalichukue”

Jery mara baada ya kuzungumza hivyo akatoka nje huku akimpigia simu Shani.

“Haloo”

“Jery mbona hunitafuti jamani mpenzi wangu. Ehee?”

“Nilikuwa nje ya Dar es Salaam. Niambie ni habari gani muhimu huyo?”

“Jery nina mimba yako”

Shani alizungumza kwa furaha sana ila kwa Jery ikawa kama ni pigo kwani alisha apa kwamba akirejea jijini Dar es Salaama ata yasitisha mapenzi yake na Shani pamoja na mama yake mkwe ili abaki na mkewe wa ndoa peke yake tu.



“Jery una nisikia mpenzi wangu?”

Shani alizungumza kwa kwa suati ya furaha iliyo pitiliza.

“Yaaa nina kusikia”

“Mbona una zungumza kama huna furaha?”

“No yani ni bonge moja ya suprize”

“Ndio baby am so happy. Njoo basi nyumbani leo”

“Ngoja niangalie utaratibu kisha nita kujulisha”

“Sawa mume wangu”

Jery akakata simu huku mapigo ya moyo yakimuenda kasi sana. Akajikuta akijipangusa jasho huku akiendelea kutafakari ni maisha gania mbayo yata mpata mtoto huyo. Akakumbuka sentensi moja ya Julieth akimueleza enedpo ata gundua kama ana msichana ana chepuka naye ni lazima ata muua.

‘Mmmm alizungumza akiwa yupo seriously sana’

Jery aliendelea kuiwazia sentensi hiyo ambayo kwa namna moja ama nyingine ime kuwa ni ngumu sana kwake. Akafungua begi haraka haraka na kutoa begi hilo na kurudi ndani.

“Jamani nina ombeni nitoke mara moja. Kuna rafiki yangu ana tatizo mahali nina kwenda kumuona”

Jery alizungumza huku akimtazama baba yake pamoja na Julieth.

“Ana tatizo gani?”

Raisi Mtenzi aliuliza.

“Ahaa ni mambo yake ya kifamilia. Kidogo kuna misunderstanding zime tokea kwenye familia yake hivyo nina kwenda kuzungumza naye. Pia ni miongoni mwa wanashauri wangu”

“Baby huyo rafiki yako ana itwa nani?”

“Aha….Msulwa”

“Sawa usichelewe kurudi mume wangu.”

“Usijali mke wangu”

Jery akambusu Julieth kwenye lispi zake.

“Baba nita ondoka na Dev peke yake”

“Sawa, sehemu unayo kwenda si ni sehemu salama?”

“Yaa”

“Sawa”

Jery akatoka ndani na kumpigia simu Devi na kumuomba aweze kuandaa gari.

“Vipi mbona haraka haraka kwema kaka?”

Devi aliuliza huku akimtazama Jery anaye onekana kutawaliwa na wasiwsi mwingi sana.

“Kaka sio salama”

“Kuna nini?”

“Shani amenipigia simu kwmaba ni mjamzito”

“Ohooo!!”

“Yaani ame nivuruga sana. Hembu washa gari twende”

Devi akamtazama Jery kwa sekunde kadha kisha wakaianza safari ya kutoka eneo hilo.

“Nina uta fanya kaka?”

“Yaani sijui. Au nimuambie atoe”

“Hapana asitoe mimba”

“Mke wangu akijua ata niua aise?”

“Mmmm ina kuwaje una muogopa mke wako kiasi hicho?”

“Sio kwamba nina muogopa. Ila nina hitaji kuhakikisha kwamba familia yangu nina iweka katika mazingira mazuri. Sihitaji tena mchepuko wa nje”

“Sasa ndio ime tokea. Hembu tuliza akili ndugu yangu. Hakikisha kwamba humuonyeshi Shani kwamba una wasiwasi na ujauzito wake. Sasa hakikisha kwamba una mpa furaha na kumuandaa mwanao. Una kwenda kuwa baba mskaji wangu”

Devi alizungumza huku uso wake ukiwa ume tawaliwa na tabasamu kwa maana leo ndio ana mshuhudia Jery akiwa na wasiwasi namna hiii. Wakafika nyumbani kwa Shani na moja kwa moja akaelekea ndani. Shani akamkumbatia kwa nguvu Jery huku akimpiga mabusu motomoto.

“Nashukuru kwa kuja mume wangu”

“Asante, ehee niambie ume pima lini?”

Shani hakujibu kitu chochote zaidi ya kuingia chumbani. Akachukua kipimo cha ujauzito na kutoka nacho na kumkabidhi Jery, ambaye alijikuta akitoka kwa macho huku akiwa kama haamini kile anacho kiona.

“Mungu amesikia kilio chako mume wangu nina kwenda kuwa mama”

Shani alizungumza pasipo kujua ni jinsi gani Jery anavyo pitia katika kipindi cha wasiwasi na woga.

“Badilisha nguo twende hospitalini”

“Sawa mume wangu”

Shani akaingia chumbani na kumuacha Jery sebleni, akiendelea kutazama kipimo hicho kilicho na vimishale viwili vyekundu.

“Tayari”

Shani alizidi kuzungumza kwa furaha. Wakatoka ndani na kuingia kwenye gari.

“Nipeleke kwa daktari wangu”

“Sawa”

Devi akawasha gari na wakaondoka.

“Mume wangu mbona kama huna furaha?”

“Ninayo furaha mke wangu. Una jua sikutarajia kama una weza kupata ujauzito kwenye kipindi hichi ikiwa uliniomba uweze kupata muda”

“Ndio hivyo mume wangu. Mungu ameweza kujibu majibu yetu”

“Ni kweli”

Devi alijihisi kucheka kwa maana laiti kama Shani angefahamu ni kitu gani kinacho endelea moyoni mwa Jery basi hata asinge furahia kiasi hicho. Wakafika hospitalini na Jery akaomba kuzungumza na daktari wake wao wawili na akanza kumueleza jinsi mahusiano yake na Shani yalivyo anza na chanzo cha kumpatia mwanamke huyo mjamzito.

“Una jua hapo tatizo sio wewe?”

“Kwa nini una sema hivyo dokta?”

“Tatizo ni mke wako alivyo kataa kubebe ujauzito kwenye kipindi ambacho wewe ulikuwa una hitaji. Ngoja nikuambie kitu kimoja ndugu yangu. Sisi wanaume huwa tukiwa katika uhitaji wa jambo fulani hususani la mapenzi. Miili yetu, mawazo yetu na mioyo yetu huwa ina kuwa ipo tayari kufanya jambo lolote kuhakikisha kwamba una kidhi hamu yako. Haijalishi utapewa na mke wako au mwanamke wa nje, ila jambo la msingi ni kwamba una hitaji kukudhi haja yako. Nipo tayari kukulindia hii siri”

“Sawa dokta hembu mpime na uniambie mima ina kipindi gani. Si una jua hawa wasichana, wana weza kubeba mimba za watu wengine na wakakupakazia wewe kutokana labda ame ona kajiuwezo kaka mnogea”

“Usijali kaka, kama haito kuwa sio yako nita kuambia”

“Shukurani sana”

Jery akatoka ofisini hapo na kumuita Shani na wakaingia kwa pamoja. Utaratibu wa vipimo ukaanza na kweli Shani akakutwa na mimba ya wiki tatu kasoro siku mbili kutimia mwezi. Kumbukumbu za Jery zikarudi nyuma kwa kasi na kukumbuka hizo siku ni zile alizo mpeleka Shani kwenye jumba la gorofa alilo nunu kwa mzungu.

‘Ohoo Mungu wangu, mimba ni yangu’

“Hongera sana ndugu yangu”

“Nashukuru sana kaka”

“Shemeji hongera nawe”

“Asante sana dokta nani una itwa?”

“Richard, Richard Msulwa”

“Asante sana”

“Ahaa….Shani kuanzi clinic zote uta kuwa una zipata kwenye hospitali hii na daktari ata endelea kukuhudumia hadi pale utakapo jifungua”

“Sawa mume wangu”

“Ila nime mueleza kwamba haya matibatu yatakuwa ni ya siri sana. Mke wangu asifahamu na wala wewe sinto hitaji uzungumze chochote kwa mtu yoyote juu ya hiyo mimba”

“Usijali mume wangu nina elewa kila kitu”

Shani na Jery wakaaga na kuondoka hospitalini hapo na kuelekea nyumbani kwa Shani.

***

“Baby nime ipata namba ya nabii Sanga”

Leila alizungumza huku wakianza kupata chakula cha usiku alicho kiandaa.

“Sema kweli?”

“Haki ya Mungu vile.”

“Ume ipatia wapi?”

“Yule rafiki yangu ambaye ana itwa Caro kumbe ana mahusiano na nabii Sanga bwana”

“Haki ya Mungu huyu mzee, ehee ikawaje?”

“Alimpigia mbele yangu akanihadithia walivyo kutana, alipo iacha tu namba yake ambayo alipiga pale nami nikiwepo, basi nikakremisha haraka haraka na tunayo”

“Basi ni moja ya ushindi kwetu. Sasa kitu cha kufanya sasa ni kuhakikisha kwamba tuna simama kwenye mpango wetu”

“Sasa ule mpango si uta kuwa ni hatari sana mume wangu”

“Usijali mimi nita kulinda na hakuna kitakacho haribika”

“Sawa nina kuamini sana Gorge wangu. Vipi leo una lala hapa nyumbani kwangu?”

Evans akajifikiria kwa sekunde kadhaa huku akimtazama Leila aliye jifunga kanga moja ambayo ni mtego tosho kwa Evans.

“Yaa nita lala hapa”

“Waoo nashukuru mume wangu”

“Shemeji yangu yupo wapi?”

“Ame kwenda kwa bwana wake huko ata rudi kesho”

“Basi sana, nita lala hapa”

Evans na Shani wakaendelea kula taratibu huku kila mmoja akimtazama mwenzake kwa macho yaliyo jaa matamanio ya kimapenzi.

***

“Yaani toka mtambue George ume kuwa ni mtu wa furaha sana”

Josephine alizungumza huku akimtazama Magreth.

“Yaani sijui yule kaka ame niroga”

“Akuroge kwani ana kuja. Wewe mwenyewe ndio ume jiroga kwake. Ila kuwa makini sana na yule kaka”

“Kwa nini?”

“Nime sema tu uwe makini naye kwa maana mtu kumuambia rafikiyako kuwa makini na mtu fulani, ni jambo zuri”

“Usijali nipo makini naye. Sana ila nina kuomba uni saidie jambo moja”

“Jambo gani?”

“Nina kuomba umuombe Mungu atusaidie kufahamu kama yule ata kuwa ni mwanaume wangu wangu au laa?”

“Sawa nita fanya hivyo, kwa maana sinto penda kukuona una huzunika moyoni mwako. Alafu kama litakuja ni jibu baya basi pia ulipokee”

“Jamani Joseee kwani huwezi kuomba nikapewa jibu zuri zuri?”

“No una jua kila unachho muomba Mungu na anacho kujibu ni kitu sahihi, yeye hawahi wala achelewi katika kujibu kwake. Hivyo ina kupasa uweze kuwa tayari kwa kila jambo”

“Mmmm haya bwana”

“Hembu mpigie”

Magreth akaitafuta namba ya Evans na kumpigia, kwa bahati mbaya akakuta simu hiyo ikiwa haipatikani hewani.

“Ohoo hapatikani”

“Ila Magreth tambua yule kaka ana mtu wake”

“Nani?”

“Si yule msichana?”

“Haki ya Mungu nita mteka yule msichana”

“Alafu”

“Awe wangu”

“Acha uchizi hata hivyo Mungu hawezi kukubariki kwa satili hiyo”

“Mimi nime mpenda sasa kwa nini awe na wasichana wengine sasa?”

“Ume mpenda wewe, yeye je ame kupenda. Hembu acha basi hiyo hali ya kupenda sana huko unapo taka kuelekea ni kutafuta matatizo mengine s……”

Gafl Josephine akaka kimya kwa sekunde ishirini kisha akafumba macho yake. Magreth hakumsemesha kitu chochote kwa maana akiwa katika hali kama hiyo basi ana tambua kuna vitu anavyo onyeshwa. Baada ya dakika tano akafumbua macho yake huku akiwa na wasiwasi mwingi sana.

“Kuna nini?”

“Twende ikulu sasa hivi”

“Niambie kuna nini?”

“Wewe twende tuta zungumza njiani”

Wakatoka nje na kufunga nyumba yao. Wakaingia kwenye gari na moja kwa moja wakaianza safari ya kuelekea ikulu.

“Ehee niambie umeonyeshwa nini?”

“Nime onyeshwa Wamarekani wana usaka ule mkataba ambao waliingia na Bokoharamu.”

“What, wame juaje kama sisi ndio tume kwenda kuisambaratisha ile kambi?”

“Wana uwezo wa kupeleleza hivyo wana tambua kwamba ni sisi ndio tume husika na wanacho kihitaji ni mkataba huo ili kuficha ushahidi”

“Sasa wata upataje?”

“Wata mtumia mtu wa ndani wa ikuku kuhakikisha wana upate ule mkataba na isitoshe ni lazima mtu huyo ata mwaga damu ya mtu ili kuupata”

“Mmmm!! Huyo mtu ni nani?”

“Hata sifahamu ila nime ona kuna mtu ata uwawa ili mkataba uweze kupatikana. Hembu goja niombe”

“Sawa”

Magreth akaendelea kuendesha gari hiyo kwa mwendo wa kasi huku Josephine akiendelea kumuomba Mungu, wakafika ikulu. Wakafunguliwa geti na kuingia ndani. Magreth akamtazama Josephine aliye fumba macho yake tu. Baada ya dakika tano Josephine akafumbua macho yake.

“Ume ona nini?”

“Twende kwa raisi”

Josephine alizungumza huku akiwa wa kwanza kushuka ndani ya gari. Wakamuuliza mmoja wa walinzi wa raisi Mtenzi na akawaleza kwamba raisi yupo nyumbani kwake. Wakaeleka nyumbani kwa raisi na kumkuta akiwa sebleni akizungumza na Julieth. Wakasalimiana kisha wakakibishwa wake.

“Muna tumia vinywaji gani?”

Julieth aliuliza huku akiwatazama Magreth na Josephine.

“Maji tu yana tosha”

Magreth alijibu. Julieth akaondoka sebleni hapo na Josephine akashusha pumzi nyingi sana huku akimtazama raisi Mtenzi usoni mwake.

“Vipi kuna tatizo Jose?”

Raisi Mtenzi aliuliza huku akimtazama Josephine.

“Ndio muheshimiwa. Kwanza sahamani kwa kuja kwako pasipo taarifa”

“Usijali. Ehee niambie ni nini?”

“Muheshimiwa ule mkataba upo?”

“Mkataba upi?”

“Wa boko haramu pamoja na nchi ya Marekani?”

“Ndio upo, vipi?”

Julieth akaweka glasi mbili za maji mezani kisha akaka kwenye sofa alilo kuwa ame keti.

“Nime weza kuonyeshwa. Wamarekani wana utafuta mkataba ule na wapo tayari kutoa kiasi kikubwa sana cha pesa katika kuupata. Mmoja wa watu wako wa karibu sana ndani ya hii ikulu ndio ata pokea dili hilo kwa siri na mtu huyo kabla ya kuuchukua mkataba huo basi ata kupiga risasi ya kichwa na atauchukua na kutokomea pasipo julikana”

Raisi Mtenzi akastuka snaa huku mapigo yake ya moyo yakimuenda kasi. Hata Julieth na Magreth nao wakajawa na mstuko sana kwa maana habari hiyo ni ya kutisha sana na isitoshe anaye tekeleza agizo hilo ni mtu wa karibu sana na raisi Mtenzi.

**************************************************


“What? Ni nani huyo ata tekeleza?”

Julieth alihoji akiwa na mshangao mkubwa sana.

“Sijaonyeshwa ni nani ambaye ata tekeleza hilo jambo. Ila kuanzia hivi sasa muheshimiwa raisi ina kupasa uwe makini kuliko siku zote ambazo ume wahi kuwa makini kwenye uongozi wako”

Josephine alizungumza kwa msisitizo.

“Mmmmm”

Raisi Mtenzi alizungumza huku akisimama kwa maana habari hiyo ina mufanya hadi ahisi utumbo wake ukimcheza kwa ndani.

‘Yaani mtu wangu wa karibu ata niua, tena ndani ya ikulu. Sasa ni wapi salama ehee Mungu wangu, ni wapi kwa kukimbilia? Nani nimu amini?”

Raisi Mtenzi aliwaza akilini mwake huku akijaribu kuwawazia mzee Mbogo pamoja na mr the Brain kwa mana ahao ndio watu wake wa karibu sana kulipa watu wote ndni ya ikulu na ndio watu wake wanao fahamu mambo mengi sana yanayo muhusu yeye kuliko watu wengine wote.

‘Kama wenge kuwa wana hitaji kunia wangesha niua. Kwa nini sass?’

Raisi Mtenzi aliendelea kuwaza.

“Josephine huyo mtu ni mwanamke au mwanaume?”

“Sifahamu muheshimiwa”

“Baba mtu wako wa karibu ni nani?”

Julieth aliuliza huku akimtazama raisi Mtenzi usoni mwake.

“Ehee?”

“Watu wako wa karibu ni nani na nani?”

“Ni….ni Brain na Mbogo?”

“Hao tu wawili?”

“Ndio”

“Ina bidi macho yao sasa tuyaweke kwao au muna semaje jamani”

Julieth aliuliza huku akiwatazama Josephine na Magreth.

“Hapana ni watu wangu wa karibu sana, ambao nime fanya nao mambo mengi sana n anime weza kuwakosea mambo mengi sana. Kama ingekua ni jambo la kuniua basi wange niua muda mrefu sana”

Raisi Mtenzi alizungumza kwa msisitizo, Magreth akamkodolea macho Josephine ambaye ameyafumba macho yake, na kuwafanya watu wote kumtazama Josephine. Baada ya dakika mbili akayafumbua macho yake.

“Nime weza kuonyeshwa huyo mtu ambaye ata husika na jambo hilo”

Kwa haraka raisi Mtenzi akaka kwneye sofa huku akiwa makini san akuweza kumsikiliza Josephine.

“Nime pewa sifa zake. Moja ni mtu ambaye ana miliki kundi kubwa la majasusi ambao waliniteka mimi. Kikundi cha mtu huyo kina husiana na uuzaji wa madawa ya kulevya, mtu huyo ndio alite husika na kuichonganisha serikali pamoja na Al-Shabab na mwisho mambo yakawa kama yalivyo tokea”

Mapigo ya moyo ya Josephine yakaanz akumuenda kasi sana kwa maana sifa zinazo tajwa zina endana kabisa na sifa zake, ila akajikaza ili kuto onekana kwamba anaye zungumziwa hapo ndio yeye.

“Mtu mwenyewe sio mwanaume ni mwanamke?”

“Mwanamke?”

Raisi Mtenzi aliuliza kwa mshangao mkubwa sana huku kwa upande wa Julieth akihisi akishikwa na tumbo la gafla la haja kubwa.

“Ndio muheshimiwa”

“Sasa ni nani jamani?”

Raisi Mtenzi alihoji huku akihisi kuchanganyikiwa.

“Sija pewa sura yake halisi. Ila hizo sifa zake ndio hizo nilizo pewa. Ina bidi kuhakikisha muheshimiwa una kuwa makini sana na wana wake wa hapa ikulu”

“Nashukuru sana kwa taarifa yako Josephine. Nina imani Mungu ni mkubwa na ata tusaidia katika hili”

“Sawa muheshimia. Nina omba tuweze kuwaacha”

“Mbona mapema”

“Hakuna muheshimiwa. Kesho ni siku ya kurudi kazini hivyo tuta zungumza mambo mengi sana tukiwa ofisini”

“Sawa nina shukuru kwa taarifa hiyo”

Magreth na Josephine wakaondoka eneo hilo na akabaki raisi Mtenzi pamoja na Julieth.

“Baba hili jambo ni hatari sana”

“Ni kweli ni jambo la hatari ila ina bidi tuwe makini sana. Alafu kuna kitu nina hitaji unisaidie”

“Kitu gani baba?”

“Nina kuomba uanze kujenga urafiki na wasichana wenye wathifa wathifa hapa ikulu na uwe nao karibu sana kwa maana nina hitaji kufahamu huyo mwanamke mwenye hizo sifa ni nani”

Raisi Mtenzi alizungumza kwa sauti ya chini pasipo kufahamu kwamba bucha lake ame mkabidhi chui aliye jivisha ngozi ya kondoo.

***

Asubuhi na mampema Leila akaelekea kazini kwake huku Evans akarudi hotelini. Akabadilisha nguo kisha akampigia dereva taksi aliye mpatia namba ya simu akitokea uwanja wa ndege. Baada ya nysu saa dereva akafika hotelini hapo.

“Habari za toka majuzi bosi”

Dereva alizungumza kwa kuchangamka sana.

“Salama habari ya wewe?”

“Salama aisee, vipi Tanzania ume ionaje?”

“Joto kali aisee. Ila nina mshukuru Mungu”

Evans alizungumza huku akiwa amekaa siti ya nyuma ya taksi hiyo.

“Wapi kaka?”

“Leo nina hitaji uweke mafuta mengi sana kwa maana kuna sehemu nyingi nyingi nina hitaji unipeleke”

“Sawa sawa, wapi una hitaji twende”

“Tuanzie kigamboni.”

“Sawa”

Wakaondoka hotelini hapo na kupita kwenye moja ya sheli, dereva akajaza tanki nzima ya mafuta na kuelekea Kigamboni. Wakafika katika eneo ambalo Evans alinunua kwa ajili ya kutengeneza kanisa kubwa. Akashuka kwenye taksi na kuanza kulikagua eneo hilo huku dereva akiwa amekabaki ndani ya gari.

“Kazi yangu ikiisha nita jenga jumba kubwa hapa. Kikubwa ni kuipata hiyo hadhina”

Evans alizungumza kimoyo moyo huku akitazama eneo hilo jinsi lilivyo kubwa. Akatoa simu yake na kupiga baadhi ya picha, kabla hajairudisha simu mfukoni, akaitafuta namba ya Magreth na akampigia.

“Haloo Geogre”

Magreth alizungumza kwa furaha sana kwa maana hakutarajia kupigiwa simu.

“Upo wapi?”

“Nipo kwangu?”

“Kwako ni wapi?”

Evans alijifanya kama hafahamu chochote.

“Kwangu ni Kigamboni.”

“Ohoo na mimi nipo Kigamboni kwa sasa. Una weza kuni elekeza niweze kufika kwako?”

“Yes waoo karibu sana”

Magreth akaanza kumuelekeza Evans ni wapi anapo ishi pasipo kufahamu Frank ni mwenyeji kabisa wa nyumba yake.

“Nita fika hapo baada ya lisaa moja na nusu hivi”

“Sawa sawa basi acha nikuandalie chakula”

“Nina shukuru”

“Usijali mpenzi wangu”

Evans akakata simu na kurudi ilipo taksi na akaingia ndani.

“Kaka hili eneo lako nini?”

“Yes so una jua kuwekeza kwenye ardhi ni jambo zuri”

“Ni kweli kaka. Hongera sana”

“Nashukuru”

“Wapi tuelekee”

“Nahitaji uni peleke kwenye moja ya hoteli hapo tukapate kinywaji kabla ya kuendelea na ratiba nyingine pia kuna kazi nita hitaji nikupatie”

“Sawa sawa kaka”

Wakafika kwenye moja ya hoteli na kutafuta sehemu iliyo tulivu na kuketi.

“Kaka una jua hii hoteli ni ya nabii Sanga”

“Wee!!”

“Haki ya Mungu vile ni nyumba ya nabii wetu, yaani ana pesa nyingi sana yule mzee”

“Aisee kajitahidi kwa kweli”

Wakahudumia vinywaji na kuanza mazungumzo.

“Nina hitaji kuwa karibu na huyu nabii Sanga una weza kunisaidia katika hilo?”

“Mmmm kwa mimi sina ukaribu sana na yule mtumishi. Ila mke wangu ni mmoja wa wahudumu katika lile kanisa na nina imani ana weza kuwa karibu sana na nabii Sanga.”

“Ahaa sasa nita hitaji jambo moja”

“Jambo gani?”

“Kuna sehemu nita pitia, sifahamu nita kaa kwa muda gani ila leo hii nita hitaji niweze kuonanana mke wako aweze kunitambulisha kwa nabii Sanga”

“Sawa kaka nita fanya hivyo ila nina hitaji kufahamu ni sababu gani haswa ina kufanya uwe karibu kuwa na nabii Sanga.”

“Biashara kama nilivyo kueleza hapo awali. Kwa msaada huo nita kupatia milioni moja”

“Hivyo tu kwa milioni moja?”

“Ndio”

“Basi sawa, hakuna saka kaka nita mueleza mke wangu kisha ata nipa ratiba kama leo nabii Sanga yupo kanisani basi nita kujulisha”

“Sawa”

Wakakaa hapo hotelini kwa nusu saa kisha wakaelekea nyumbani kwa Magreth. Evans akamlipa dereva huyo laki mbili na kumuahidi ata mpigia simu akimaliza kuzungumza na mwenyeji anaye kwenda kumuona ndani ya hiyo nyumba.

“Shukrani sana kaka”

Dereva huyo aliye jitambulisho kwa jina la John alizungumza kwa furaha sana kwa maana mizunguko hiyo michache ime weza kumpatia pesa nyingi tena kwa asubuhi hiyo. Isitoshe akilini mwake ana iwazia milioni moja atakayo pewa na Evans kama ata ikamilisha kazi hiyo. Evana akaminya kengele huku akitazama kamera iliyopo hapo geti. Hakika mazingira na nyumba hiyo hayaja badilika sana. Geti likafunguliwa na Magreth akakumbatia Evans kwa furaha sana huku akimpiga mabusu mfululizo ya mdomoni.

“Karibu sana kwangu mume wangu”

Magreth alijikuta akiropoka pasipo kuja kama jibu lale kwa kijana huyo ni ndio au hapa.

“Nina shukuru sana”

Wakaingia ndani na Magreth akamkaribisha kwa furaha, Evans akaendelea kutazama eneo la nyumba hiyo, akakumbuka kipindi alipo kuwa ana fukuzwa na nabii Sanga.

“Rafiki yako yupo wapi?”

“Ame kwenda kazini.”

“Oohoo kwa hiyo upo peke yako?”

“Yes baby, nina imani una njaa. Nime kuandalia chakula kitamu sana, karibu sana mezani”

“Nina shukuru”

Wakakaa kwenye viti vilivyo izunguka meza hiyo. Magreth akaanda chakula hicho ambacho ni ndizi na nyama. Wakaanza kula taratibu huku Evans akisikilizia utamu wa chakula hicho.

“Aisee una chakula kitamu sana”

“Nashukuru baby”

“Ehee hembu niambie maisha yako ya nyuma ya mahusiano ilikuwaje kuwaje, hadi ukatengana na boyfriend wako?”

Evans alizungumza kwa suti ya upole huku akimtazama Magreth usoni mwake aliye jikuta akiaha kula kabisa na kukaa kimya kwa sende kadhaa.

“Sitaki kukudanganya kitu, naogopa nikikudanganya na baadae uka fahamu nina imani kwamba nita kuw akwneye hali mbaya.”

“Yes niambie tu ukweli?”

Magreth akamimina maji kwenye glasi na kuyanywa nusu glasi ilikulainisha koo lake kwani anayo kwenda kuyazungumza kuna mambo mengne ni magumu na mazito na mengine ni mepensi hivyo ni lazima ahakikishe ana liweka sawa koo lake.

“Kipindi nipo masikini, sina hizi mali au haya mafanikiioo nilikuwa nina uza maandazi ya kutembeza kwenye mitaani kwenye deli. Hiyo biashara niliweza kuachiwa urithi na mama yangu na nilijitahidi kuifanya huku nikiamini kwamba ipo siki Mungu ana weza kunifanikisha na kunitoa katika biashara hiyo.”

Magreth alizungumza kwa sauti ya upole sana huku akimtazama Evans anaye anaye mjua kwa jina la Gorge usoni mwake.

“Basi siku moja alfajiri na mapema sana nilikuwa kwenye vichochoro vyetu kule Mazense. Basi nilikutana na vibaka ambao mmoja wa wale vibaka, mkuu wao alikuwa ana nitongozaga kipindi cha nyuma ila mimi nilikuwa nina mkataa kwa maana nilikuwa ni msichana mwenye msimamo na hofo ya Mungu kwa maana nili jiapiza moyoni mwangu kwamba usichana wangu ata kuja kuutoa mwanaume ambaye nita mpenda na ita kuwa ndio zawadi yangu kwake.”

“Mambo yalikuja kuvurugika asubuhi moja nilipo kutana na vibaka hao. Walianza kunigasi huku wengine wakianza kunishika shika. Japo nina uwezo mkubwa sana wa kupigana ila nilijikuta nikiwa mstahimilivu ili kuangalia wata ishia wapi. Nikiwa nina jiandaa kupambana nao, akatokea kijana mmoja ambaye huyo ndio aliye uteka moyo wangu”

Magreth akakaa kimya huku akitoa tabasamu la kiunyonge.

“Yule kijana alianza kupambana na wale vibaka ili kuniokoa mimi. Nikiwa nimeshikwa na bumbuwazi mmoja wa vibaka ali mchoma kisu yule kijana na wakakaimbia”

“Huyo kijana ana itwa nani?”

“Evans, Evans Shika”

Mwili mzima wa Evans uka sisimka kwa maana Magreth ana lifahamu hadi jina lake la ukoo na hajalisahau kabisa.

“Ilinibidi nimkimbize hospitalini. Madaktari wakaniambie nifwatilie kibali polisi, nikafanya hivyo na nikapewa RB ya kuwasaka wale vijana. Nika rudi hospitalini na kukuta kijana yule akiwa ameingizwa ndani ya chumba cha upasuaji. Niliogopa sana na niliumia sana. Nilitoa akiba yangu ndani yote ila haikuweza kutosha kwa maana ilikuwa ni ndogo.”

“Sikuweza kuwafahamu ndugu wa Evans hivyo ilinilazimu kuanza kutafuta pesa kwa watu ninao wamudu, ila kila mmoja aliweza kunipa sababu zake. Kila mmoja hakuweza kuniamini kwa maana wana amini fika sina uwezo wa kulipa hicho kiasi. Ndipo nilipo mkumbuka aliye kuwa baba yangu wa kiroho nabii Sanga”

Magreth akaka kimya kwa sekunde kadhaa huku akimtazama Evans usoni mwake.

“Nilivyo dhani ndivyo, kumbe sivyo. Yule mzee hakuwa ni mtu wa Mungu kama wengu tunavyo muona kwenye macho ya watu. Kwani alitumia ushawishi wake wa pesa kunihadaa na akatumia kigezo cha kumsaidia Evans kama njia ya kuhitaji kitu kwangu kwani ilikuwa ni kama nipe, nikupe”

“Una maanisha nini?”

“Yule mzee alinieleza ili kumsaidia mwanaume huyo ilibidi nimpatie penzi. Sikuwa na jinsi na namna wala pesa ya kumsaidia Evans wa watu hivyo nilijikuta nikiuza usichana wangu kwa ajili ya kupona kwake. Japo niliumia sana tena sana ila sikuwa na jinsi zaidi ya kuhakikisha nina fanya maamuzi magumu kwa ajili ya Evans ambaye kuanzi ile siku nilitokea kumpenda sana. Nilichelewa kumueleza ukweli wa mambo ndio maana ilifikia hatua ya yeye kuniacha na kuondoka mbali na mimi na siku hiyo ndio siku ambayo nilipata ajali nikiwa na huyu rafiki yangu katika harakati za kumuokoa Evans mkoani Morogoro alipo kuwa ame tekwa na watu wasio julikana.

Evans akajikuta akistuka kidogo kwa maana hakutambua kwamba siku ambayo alitekwa na watu wa Jerykumbe Magreth na Jospephine walikuwa wana mfwatilia.



“Aisse kwa hiyo mara baada ya kupata ajali ilikuwaje?”

Evans aliuliza hukua kihitaji kujua zaidi juu ya jambo hilo.

“Hatukuwa na uwezo wa kuendelea kwa maana rafiki yangu alivunjika mguu na gari ilipinduka hivyo kilicho kuwa kime baki ni kuhakikisha nina mpatia huduma rafiki yangu. Kuanzia siku hiyo sikuweza kupata nafasi ya kumuona Evans. Nilijikuja kuonana naye siku za mlipuko wa mabomu hapa Dar es Salaam. Na nilimuona akiwa na msichana mwengine. Hakika moyo wangu uliumia sana na mbaya zaidi rafiki yangu aliniambia kwamba yule msichaa ni jini ambaye ana msaidia Evans”

Evans akastuka kidogo ila akaficha mstuko wake huo kwa maana haitaji Magreth agundua chochote.

“Aisee”

“Yaa basi penzi letu liliishia hewani kama hivyo. Ila mtu pekee ninaye mlaani kwenye hili ni nabii Sanga kwa maana alipoteza ndoto za mwanaume ninaye mpenda”

“Pole sana”

“Nashukuru”

“So kwa hiyoEvans bado ana ishi moyoni mwako?”

Swali la Evans likamfanya Magreth kushusha pumzi nyingi huku akitafakari namna ya kujibu swali hilo.

“George”

“Naam”

“Kusema kweli upendo wa Evans bado upo moyoni mwangu. Ila nilipo kuona wewe nilihisi hisia kama zile nilizo wahi kuzipata kwa Evans. Nilishindwa kujizuia na kuuzuia moyo wangu kukupenda, sijui ni kitu gani kilicho tokea hapa katikati, ila ukweli ndio huo. Kusema ukweli ume weza kuuchukua upendo wa Evans moyoni mwangu”

“Ngoja kwanza Magreth ina maana kama akitokea Evans sasa hivi na akatokea kukusamehe, uta mpenda?”

“Mimia ni mwanamek mwenye msimamo hususani kwenye mapenzi. Kama nitakuwa nipo na wewe hakika ita bidi kuheshimu mapenzi yangu haya mapya na kuachana naye. Ndio maana toka kipindi niachane naye na kumtoa nabii Sanga kwenye maisha yangu hakika sikuhitaji kuwa na mwanaume tena kwenye maisha yangu”

“Kweli?”

“Haki ya Mungu vile, sikuwahi kuwa na mwanaume mwengine na nilijiapiza sinto kuwa na mwanaume hadi pale moyo wangu utakapo pata mtu nitakaye mpenda kama nilivyo mpenda Evans. Mtu mwenyewe ni wewe, hakika nina kupenda sana George”

Magreth alizungumza kwa sauti laini iliyo jaa mahaba ndani yake. Taratibu akasimama na kumsogelea Evans kwneye kiti alicho kaa na kumshika mkono wa kulia na kumnyanyua kwenye kiti.

“George, mimi sio malaya. Kukupenda kwangu kume toka moyoni na wala usichangae kuona nime fungua hizia zangu kwako. Kusema ukweli ni kwamba nina kupenda sana”

Magreth taratibu akajisogeza kwa Evans na kumkumbatia. Chuchu za Magreth zilizo zimama vizuri zikaanza kumsisimua Evans kwa maana zina mchoma choma kifuani mwake. Taratibu Evans akashusha mkono wake kwenye kiuno cha Magreth na kuanza kukitomasa. Ulaini wa mwili wa Magreth hakika haujabadilika toka kipindi cha mwisho walipo achana. Wakaanza kupeana denda huku kila mmoja akizama kwenye hisia kali za kimapenzi. Evans akajikuta akishangaa kupata msisimko mkali sana kuliko na vile alivyo taratjia. Akambeba Magreth huku wakiendelea kunyonyana deda. Evans akafungua mlango wa chumba cha Magreth na moja kwa moja akamlaza Magreth kitandani mwake na wakaanza kuvua nguo. Jambo la kumshukuru Mungu ni kwamba makovu yate ya mwilini mwake yame muisha na hata kovo la kuchomwa kisu lime muisha, laiti kama angekuwa nalo basi inge kuwa ni rahisi sana kwa Magreth kuweza kuliona.

‘Mtoto bado ni mzuri aisee’

Evans alizugumza huku akitazama mwili wa Magreth aliye mlaza chini. Chuchu zake hakika zilizidi kumpagawisha Evans, akatazama kiuno chembemba kiasi kililicho beba hispi nene pamoja na makalio makubwa kiasi. Kwa jisni Magreth alivyo jawa na uhitaji wa mwanaume wala hakuhitaji kuandaliwa sana kwa maan tayari kitumbua chake kilisha lowana. Evans bila hiyana akanza kumshuhulikia Magreth mwaamke wake wa kwanza kuwahi kufanya naye tendo la ndoa kwenye maisha yake yote. Utamu wa Magreth hakika ume weza kuwapita wasichana wote alio wahi kuwashuhulikia.

“Aiis…a…iia..ah..u…a”

Magteh alilalama huku miguu yake akiwa ameibana kwa pamoja na ameiweka mabegani mwa Evans ambaye yupo kasi ya spidi mia na ishirini, mithili ya gari Ferrari. Hadi wana maliza mzungungo wa kwanza Magreth akaanza kuisi kitu na kwa maana mikao yote aliyo wekwa ndio mikao ambayo Evans alikuwa akimuweka kitandani, ila akshindwa kuzungumza kwa maana hakujua ni jinsi gani mpenzi wake huyo mpya atajisikia kufanaishwa na mwanaume aliye pita katika maisha ya Magreth. Hawakupumzika hata dakika kumi, Magreth akaanza uchokozi ulio mpelekea Evans kurudi mzigoni na kuanzisha mzunguko wa pili ambao huu sana ilikuwa ni babu kubwa kwani Magreth alilia vilio vya aina vyote vya raha. Chuki na sumu aliyo itengeneza ndani ya moyo wake juu ya kumuua Magreth akajikuta ikianza kuyayuka mithili ya barafu juani. Hadi wana maliza mtanange huo kila nia mbaya aliyo kuwa ameipanga moyoni mwake ikatoweka.

“Ume jisikiaje baby”

Evans aliuliza huku akiwa amejilaza pembeni ya Magreth anaye hema kwa kuchoka.

“Aisee raha sana”

“Kweli?”

“Haki ya Mungu yaani, ume nipa raha sana mpenzi wangu. Geogre nina kuomba uachane na yule binti”

Kauli ya Magreth ikamfanya Evans kukaa kitako kitandani na kumuangalia.

“Msichana gani?”

“Yule muhudumu pale wa Samaki Samaki. George mimi nina wivu na wewe na sinto kubali kukuona una endelea kuwa na yule msichana. Haki ya Mungu nita mfanya jambo baya”

Magreth alizungumza kwa msisitizo kwa maana hatamani kuona hata siku moja Evans ana kuwa na msichana mwengine.

“Nipe muda”

Evans alizungumza kwa kifupi huku akishuka kitandani.

“Ina maana”

“Maana ya kwamba nipe muda wa kumuacha. Tambua yule ni mwanamke kama wewe na ana moyo kama wewe na yule ndio wa kwanza kuwa nami hivyo nipe muda wa kumuacha”

“Geogre kwa nini lakini una nifanyia hivyo?”

“Sio nina kufanyia hivyo. Mimi ni mtu muwazi na mkweli, sipendi kumuumiza mtu na hisia zake. Kama hutoajali nipatie muda ila endapo utajaribu kumdhuru au kuzungumza naye au kufanya jambo lolote la kijinga kwake. Nita kuacha”

Evans alizungumza kwa msisitizo na kumfanya Magreth kuwa mnyonge kwa maana neno kuachwa lime mkata maini na wala hatamani kuachana na mwanaume anaye mpenda na uzuri ni kwamba ana weza kumuhimili kitandani na kumkata haja zake zote za kimapenzi.

“Sawa baby sasa uta muacha baada ya muda gani?”

“Nita kuambia”

Evans alijibu kwa kifupi huku akiendelea kuangaza angaza nda ya chumba hichi. Akapiga hatua hadi kwenye moja ya droo ya kabati na kufungua. Akakuta baadhi ya nguo zake zikiwa zime kunjwa vizuri na kuweka humo. Magreth akastuka kwani hakuamini kama Evans angeweza kufungua kabati hilo kwani humo amezificha nguo za Evans ili nabii Sanga asizione.

“Ahaa George…”

Magreth hakumalizia kauli yake kwani tayari Evans alisha toa shati ambalo ana kumbuka vizuri. Shati hili lenye madoa ya damu ndio shati alilo kuwa amelizaa siku alipo chomwa kisu. Akalitazama kwa sekunde kadhaa shati hilo huku machozi yakimlenga lenga. Kabla Magreth hajamsogela akajikuta akijifuta machozi kisha akageuka huku akiwa amejawa na tabasamu.

“Hili shati vipi mbona lina damu?”

“Ahaa….ah…a…George”

Magreth alijikuta akijawa na kigugumizi.

“Usijali nime weza kufungua kabati bila ruhusa yako”

“Hapana hakuna shida. Hapa ni kwako na una haki ya kufanya chochote”

“Kweli”

“Ndio”

“Ehee hili shati vipi mbona lina damu?”

“Kama nilivyo kueleza sikuya kwanza kukutana na Evans ndio nilikuta na hili shati na alichomwa kisu na wale vibaka”

“Una zikumbuka sura zao?”

“Mmoja ndio nina mkumbuka”

“Nahitaji tuwatafute”

“Ehee!!?”

Magreth alishangaa kidogo kwa maana hakutarajia kama Geogre ana weza kumuambia jambo kama hilo.

“Kwa nini?”

“Nahitaji kulipiza kisasi kwa ajili ya X wako”

“Ila George mimi nilisha sahau na kuwapoteza. Jambo la kumshukuru Mungu Evans hakufa”

“Nime kuambia nina hitaji tuwatafute”

Evans alizungumza huku macho yake yakiwa yamejawa na hasira. Aina hiyo ya mikunjo ya macho yaliyo jaa hasira, ika zidi kumpa maswali mengi Magreth kwa maana hata Evans huwa akikasirika ana kuwa hivyo hivyo. Magreth akashusha macho yake taratibu hadi kwenye upande ambao Evans alichomwa kisu na kukuta hana kovu lolote.

“Why”

Magreth aliuliza kwa sauti ya upole ila yenye udadisi ndani yake kwa maana tayari machale yamesha anza kumcheza japo hana uhakika sana.

“Au basi”

Evans alizungumza huku akilirudisha shati hilo ndani ya droo hiyo.

“Hapana George. Nahitaji ufurahi na tuna weza kufanya kama ulivyo hitaji. Twende kwenye mtaa nilio kuwa nina ishi”

Evans akatazama saa ya ukutani chumbani hapo na kuona muda bado una ruhusu. Wakakubaliana na wakaingia bafuni kwa pamoja na kuanza kuoga. Magreth akajitahidi kuuchunguza mwili wa Geogre ili aufananishe na mwili wa Evans ila akashindwa kwa maana mwiliw a Geogre ume jengeka vizuri kwa mazoezi na mwili wa Evans haukuwa na misuli kwani alikuwa ni mwembamba. Wakarudi chumabani na kuvaa nguo zao.

“Kuna foleni nyingi mchana huu. Tutumie pikipiku au gari?”

“Pikikipi”

Magreth akabeba kofia mbili ngumu za pikipiki hiyo na wakatoka nje.

“Nita endesha”

Evans alizungumza na Magreth akambidhi funguo. Wakaondoka nyumbani hapo na Magreth akaanza kumuelekeza wapi waelekee. Japo mitaa hiyo Evans ana ifahamu vizuri sana ila akajifanya kana kwamba hajui ni wapi wanapo kwenda. Wakafika katika mtaa ambao hapo zamani alikuwa ana ishi Magreth. Jambo la kumshukuru Mungu, mtaa huo haukuweza kukumbwa na dhahama ya milipuko ya mabomu.

“Alikabiwa wapi?”

“Maeneo ya huku ila eneo hilo lina vichochoro ambavyo pikipiki haiwezi kupita. Labda tuiache pikipiki katika ile nyumba pale”

Magreth alizungumza huku akimuonyesha Evans nyumba aliyo kuwa ana ishi. Wakasimama katika nyumba hiyo na wakashuka.

“Dakika mbili”

Magreth alizungumza huku akipandisha ngazi za kibarazani na kuingia ndani ya nyumba hiyo na kuanza kuwasalimia wapangaji wezake ambao hakika walipo muona wakajawa na furaha nyingi sana. Hata mama mwenye nyumba naye furaha ilimtawala japo aliweza kukosana na mwana mama huyo kwenye kipindi alicho kuwa ana ishi hapo na mara ya mwisho kufika kwenye mgahawa wake.

“Jamani nina pita tu, nina acha pikipi yangu hapo nje nita kuja baadae kupiga stori na nyinyi”

Magreth alizungumza na wakatoka nje huku akiwa ameongozana na wapangaji wezake. Akamtambulisha Evans kwa wana mama hao na kueleza kwamba ni mume wake. Baada ya stori za hapa na pale wakaondoka na kuanza kupita kwenye vichochoro vya mtaa huo. Wakafanikiwa kufika kwenye kichochoro ambacho Evans alichomwa kisu.

“Eneo hili ndipo tukio lilitokea”

Evans akasimama eneo ambalo ana kumbuka alilala chini huku akiwa wana vunjwa na damu. Akachuchumaa huku akitazama eneo hilo kwa umakini sana. Akafumba macho yake na kuanza kuvuta kumbukumbu za sura za vijana ambao walimshambulia na kumuharibia mstakabali wake wa masomo kwani walikimbia na geni ambalo lilikuwa na viyambulisho vyake vya kuanzia shule ya msingi hadi chuo kikuu.

“Hembu sogea hatua mbili nyuma”

Evans alizungumza hukua kimueleza Magreth na akafanya hivyo. Magreth akasimama eneo ambali alikuwa ana letewa ghasia na vijana hao. Magreth akafumba tena macho yake na kuaza kuliona tukio zima kwenye ufahamu wake wa akili. Japo ni siku nyingi zimepita ila akafanikiwa kukumbuka sura za vijana hao. Akasiamama na kumsogelea Magreth.

“Kuna maskani ngapi katika huu mtaa unazo zijua zina kaa vibaka?”

“Mbili, moja wana jiita Turboni na nyingine wana jiita Panya Road. Ila sijajua wale jamaa walikuwa ni wa maskani gani”

“Twende kwenye hizo maskani”

“Ngoja kwanza mume wangu”

Magretha alizungumza huku akimsogelea Evans.

“Hizo maskani tunazo kwenda ni za watu walio data na maisha. Ni watu ambao wao kumuua mtu kwa kumkata kata kwa mapanga ni jambo rahisi sana”

“Ila wewe si una weza kupiga?”

“Ndio mume wangu”

“Basi uta nilinda”

Evans alizungumza huku akitabasamu na kumfanya Magreth kukaa kimya kwa sekunde kadhaa kisha wakakubaliana. Wakafika kwenye maskani ya kwanza na kukuta kundi kubwa la wavuta bangi na watumiaji wa madawa ya kulevya. Waka wahesabu kwa haraka vijana hao wa mariki tofauti tofauti huku wakiwa wame valia nguo za ajabu ajabu, na kukuta wapo ishirini na mbili. Vijana hao wakanyama mazungumzo yao huku wakiwatazama Evans na Magreth walio simama mbele yao. Wakaanza kuwatathimini mavazi yao waliyo vaa na wakatambua kabisa kwamba watu hao wana pesa.

“Hei mume potea njia au mume kuja kutuletea mavumba”

Mkuu wa maskani hiyo alizungumza huku si Evans wala Magreth aliye weza kujibu swali hilo. Kazi ya Evans ikawa ni kuhakikisha ana zitafuta sura za vijana hao wali mchoma kisu.

“Mume wangu hapa hawapo. Tuondoke zetu hawa ndio Panya road”

Magreth alizungumza mara baada ya kuwatazama vijana wote kwa umakini.

“Oya wewe choko, una kuja kuturingishia manzi wako au una taka tuwatie madol** ya mikund** ili mujue kwamba mumeingia sehemu siyo”

“Una semaje dogo?”

Evans alizungumza huku akimtazama kijana huyo aliye chomoa kisu kiunoni mwake na kukishika kwa umakini.

“Hei baby achana nao bwana tuondoke”

“Hapana hawawezi kutuzalilisha. Rudia tena una sema”

Evans alizungumza kwa msisitizo huku akimkazia macho kijana huyo.

“Kum** la mama yako, nani dogo?”

Tusi hilo likawa lime mtia wendawazimu Evans ambaye toka ametoka mafunzoni hajawahi kuchangamsha viongo vyake kwa kupigana. Gafla Evans akaruka juu na kuashia teke ziti lililo tua kifuani mwa kijaan huyo na kumfanya arushwe nyuma na kuwaangukia wezake jambo lililo wafanya vijana hao wote kusimama kwa haraka na kushika mapanga, wengine visu huku wengine wakiwa na marungu tayari kwa kumshambulia Evans na Magreth.



“Jamani hatujafwata ugomvi. Tuna ondoka”

Magreth alizungumza huku akiwatazama vijana hao.

“Waueniiiiiiiii”

Mkuu wa kundi hilo la Panya road aliwaamuru wezae kwa sauti ya kujikaza huku damu zikimchuruzika mdomoni kwa maaana teke alilo pigwa lime vuruga mfumo mzima wa kifua chake. Vijana hao kama nyuki walio furumushwa kutoa kwenye mzinga wao wa asali ndivyo jinsi walivyo anza kuwashambulia Evans na Magreth. Ila kusema kweli ikawa ni siku yao mbaya tofauti na walivyo zoea kuwavamia watu wanyonge na wasio jiweza. Mapigo ya Evans yakamuacha hoi Magreth kwa maana kila aliye pigwa hakudhubutu kusimama tena. Wapo walio vunjwa miguu wengine mikono, huku wengine walivunjwa mbavu kazaa katika miili yao. Ndani ya dakika tano, vilio vya maumivu vikatawala katika maskani ya Panya road.

“Nyau road leo nime kuja wajinga nyinyi”

Evans alizungumza huku akihema kwa maana shuhuli aliyo ifanya ni kubwa kuliko Magreth ambaye yeye ame wapiga wawili tu ambao walimvamia kwa ajili ya kumdhuru.

‘Hapa nime pata mwanaume, haki ya Mungu, mwanaume ana jimudu kwa kila kitu. Huyu sio Evans.’

Magreth alizungumza kimoyo moyo huku akiwatazama vijana hao wanao ugulia maumivi.

“Baby ngoja niwapige simu polisi”

“Hapana, tuna hitaji kwenda kwenye huyo maskani nyingine”

“Sawa basi ngoja niwarekodi, ili kama tukiwa tume toka kwenye hiyo maskani nyingine tuwape askari habari”

“Poa ila ngoja kwanza”

Evans alizungumza kisha akaanza kuwavunja miguu bila ya huruma wale wote walio bahatika kuvunjwa mikono na mbavu. Zoezi hilo likamfanya Magreth kumshangaa sana George(Evans) kwa maana ni mtu anaye onekena hana huruma hata theluthi.

“Niangalieni hii sura na ile pale. Endapo siku nyingi zita pita haya maeneo hakikisheni kwamba hamtufwati. Tumeelewana?”

“Ndi…io”

Ni mmoja tu wa vijana hao alijibu huku damu zikimtika mdomoni na puani mwake. Magreth na Evans wakaondoka eneo hilo. Wakiwa katika moja ya uchochoro wakakuta kundi jengine la vijana sita wakicheza kamari. Wanne kati ya vijana hao sita Evans aliweza kuwakumbuka ni miongoni mwa vijana walio washambulia siku ile.

“Baby wale vijana wanne nina wakumbuka”

Magreth alizungumza kwa sauti ya kunong’oneza. Vijana hao wakaanza kuwatazama Magreth na Evans wanao wakaribia.

“Oii dili hilo”

Mmoja wa vijana hao aliwaambia wezake huku wakiweza visu vyao tayari kwa kuwashambulia Magreth na Evans.

“Tuwabananishe, wewe kaa hapa”

Evans alizungumza na kumfanya Magreth asimame. Kwa kasi ya ajabu Evans akawaruka kwa sarakasi kadhaa hewani vijana hao na kutua upande wa pili wa kichochoro na kuwaweka kati vijana hao. Vijana wavili waliweza kumkumbuka Magreth kwa maana wana mfahamu vizuri.

“Aissee huyu ni yule muuza maandazi bwana”

Walizungumza kwa kejeli huku wakiwatazamaa Magreth na Josephine.

“Ohoo naona leo ume leta chakula cha bosi ehee. Yule bwege wako vipi alikufa?”

Waliendelea kumkejeli Magreth. Kitendo cha kumshambulia Evans ikaw ani kosa kubwa sana,wani wakaanza kupokea kichapo ambacho hakuna aliye kutarajia. Magreth naye hakutaka kuficha uwezo wake kwa vijana hao ambao siku zote wana mfahamu kama muuza maandazi. Kipondo cha mbwa koko walicho kipokea kilwafanya wote wasalimu amri huku wakilia. Hapakuwa na aliye na uwezo wa kurusha ngumi wala teke kwa maana wame vunjwa kisawa sawa.

“Mkubwa wenu yupo wapi?”

Magreth alimuuliza mmoja wao huku huku akiwa amevibenua vidole vya mkono wa kushoto.

“Yu…upo maskani”

“Wapi?”

“Hapo kati”

Kijana huyo alizungumza kwa kulia huku mkono wake kulia ukiwa ume vunjwa mara mbili.

“Mnyanyue atupeleke”

Evans alizungumza na Magreth akafanya hivyo. Wakaanza kukatizana naye vichochoroni hadi wakatokea uwani wa nyuma moja iliyo chakaa chakaa. Kijana huyo akasimama hadi kwenye moja ya chumba cha uwani katika nyumba hiyo ambapo mziki mkubwa sana una toka ndani ya nyumba hiyo. Kijana huyo akagonga kwa nguvu na sauti ya redio ikapunguzwa.

“Nani?”

Ilisikika sauti ya kiume ikiuliza kwa ukali.

“Mimi hapa mkuu”

“Dosi”

“Ndio ni mimi”

Mlango ukafunguliwa na akachungulia kijana ambaye Magreth na Evans walimfahamu vizuri. Kijaa huyo ndio aliye mchoma kisu Evans. Evans akamsukumia ndani kijana huyo na akaangukia kwenye meza iliyo jaa vibunda vya mirungi. Kwenye kitanda amekaa mkuu wao ambaye ameshikilia kipisi cha bangi. Magreth akamzimisha kijana wa nje na yeye akaingia ndani.

“Suprize”

Magreth alizungumza huku akitabasamu. Mkuu wao huyo akastuka sana kumuona Magreth.

“Ume fwata nini wewe demu muuza maandazi?”

“Nime kuja kukubalia ombi lako”

Kijana aliye angukia akajaribu kunyanyuka ila Evans akawahi kumpiga teke la sehemu za siri na kumfanya atoa ukelele. Magreth akasogelea redio na kuongeza sauti ili kinacho endelea ndani kisiweze kusikiwa na walio nje.

“Baby huyu ndio alikuchoma kisu na huyu ndio mkuu wao”

Magreth alizungumza huku akisimama mlangoni. Evans hakuw ana huruma, akaanza kutembeza kipigo kitakatifu na mbaya zaidi tisheti aliyo ivaa huyu mkuu wao ni miongoni mwa nguo zake walio ondoka nazo sikue ile. Evans akachukua moja ya kisu na kuanza kuwachana chana vibaja vijana hao na kusababisha damu nyingi kusambaa ndani ya chumba hicho. Sura za vijana hao zilijaa michano hiyo ya visu na kuwafanya walie sana. Evans akaona begi lake la mgongoni likiwa lime simamishwa pembezoni mwa kitanda. Akalichukua kwa haraka na kulifungua ndani. Akashusha pumzi nyingi mara baada ya kukuta vyeti vyake vikiwa havijaguswa kabisa, hapo ime pita muda mrefu sana toka akumbane na matatizo ila wame weza kumtunzia.

“Hivyo ni vyeti vya Evans”

Magreth alizungumza huku akivitazama vyeti hivyo.

“Uta mtunzia”

Evans alizungumza huku akifungua zipu nyingine za begi hilo na kukuta likiwa na vipisi vya bangi na mabunda ya mirungi. Akavitoa vitu hivyo kisha wakaondoka eneo hilo pasipo watu kuwaona na wala kugundua ni kitu gani likilicho endelea ndani hapo. Wakarudi ilipo pikipiki. Magreth akaaga kwa majirani zake na wakaondoka eneo hilo.

***

“Waooo Caro una ume pendeza sana”

Josephine alizungumza huku wakikumbatiana na Caro waliye panga kuonana kwneye mhahawa huo ulio karibu kabisa na ikulu.

“Hata wewe upo vizuri sana mpenzi. Tazama sasa una lindwa ume kuwa mtu mkubwa sana ehee?”

Caro alizungumza huku akitazama walinzi wawili walio simama eneo la karibu kabisa na alipo Josephine.

“Haha usiogope ni kawaida”

“Mmmm Josephine kawaida gani rafiki yangu. Yaani kweli Mungu akiamua kukunyanyua ana kunyanyua tu. Nakumbuka kipindi kile mimi, wewe na Magreth tukiimba kwanya kanisani kwa Sanga, yaani tukitoka hapa ni full kutembea kwa miguu”

“Hahaa umeona ehee. Ila maisha yame badilika na wewe nina kuona una ng’ara mtoto wa kike”

“Kidogo. Nashukuru kwa kukutana na mimi”

“Usijali ehee niambie kwa maana sikua amini kama wewe ndio ulinipigia. Yaani nika sema lazima leo tuonane. Hivi ulipotelea wapi?”

“Biashara rafiki yangu, kipindi kili niliamua kujikita kwenye biashara. Nina mshukuru Mungu huko ndipo nilipo weza kuyabadilisha maisha yangu”

“Mungu ni mwema”

“Ehee niambie na wewe ulifikaje fikaje ikulu”

“Haahaa ni stori ndefu sana ila jambo la kumshukuru Mungu kwa sasa nipo vizuri”

“Magreth kwa sasa naye yupo wapi?”

“Kwa sasa ata kuwepo nyumbani ila nina mshukuru Mungu na yeye ana endelea vizuri”

“Kuna kipindi niliona ame fungua mgahawa wake, nilikuwa nchini Afrika kusini hivyo nilishindwa kuja kumuunga mkono”

“Ahaa sawa sawa. Ila Caro nakuona ume kuwa mdada mkubwa mkubwa”

“Hahaa hapana bwana. Hata wewe ume kua”

“Yaani kipindi kile tuna imba kwaya ulikuwa bado kadogo dogo”

“Ndio miaka ina sogea mbele ndugu yangu na isitoshe mavyakula haya tunayo kula ndio balaa tupu”

“Ni kweli, ina bidi uanze kufanya mazoezi ili usiendelee kunenepa tena zaidi ya hapo”

“Hivi Jose ume nenepa ehe?”

“Yaa ume nenepa”

“Kama wewe ume niambia basi nita pungua. Ehee hembu niambie umesha olewa?”

“Aha…mimi bado vipi wewe?”

“Hata mimi bado. Mage je?”

“Naye bado, una jua ni miaka mitatu hatujaonana”

“Yaa ni miaka mitatu, nika hisi wezangu muta kuwa mumesha nitangulia kwenye maisha ya ndoa”

“Ahaa bado aisee. Ila Mugu ni mwema ata tusaidia”

Caro na Josephine wakaendelea kuzungumza mambo mengi sana waliyo yafanya kwenye urafiki wao. Josephine akamuelekeza ni wapi wanapo ishi yeye na Magreth na kuahidi kwamba siku itakayo fwata ata watembelea. Baada ya lisaa wakaagana na Josephine akawa wa kwanza kuondoka kwenye mgahawa huo akiongozana na walinzi huku Caro naye akiingia kwenye gari lake. Kabla ya kuwasha gari akamitafuta namba ya nabii Sanga na kumpigia.

“Haloo”

“Ndio”

“Nime onana na Josephine na mambo yana kwenda vizuri.”

“Safi sasa sasa hakikisha una zidisha ukaribu nao na kufahamu kila kinacho endelea”

“Sawa mume”

“Poa nita kupigia”

“Sawa”

Caro akakata simu na kuondoka eneo hilo huku akiwa amejawa na furaha kwa maana pesa alizo ahidiwa na nabii Sanga hakika ni nyingi sana kama akifanikiwa kuifanya kazi aliyo pewa vizuri sana.

***


ITAENDELEA



0 comments:

Post a Comment

BLOG