Search This Blog

Wednesday, November 18, 2020

SIN SEASON 2 SEHEMU YA 2/10

   


SIN SEASON 2

WRITER…………………………………………EDDAZARIA G.MSULWA
WEBSITE………………………………………… www.storyzaeddytz.com
CONTACT……………………………………….. 0657072588/0768516188
AGE……………..18+

SEHEMU YA 2 KATI YA 10


“Kuna mtu alipanga kumuua raisi Mtenzi hivyo hapa malaika wa Mungu wame niambia kwamba ata kuja kuonakana akiwa na afya yake njema na ata rudi kuiongoza serikali yake kwani yey ndio chaguo sahihi la mwenyezi Mungu”

Makamu wa raisi mapigo yake ya moyo yakampasuka mithili ya mftuza lililo chomwa na pini. Mapigo yake ya moyo yakazidi kuchanganya, akahisi kijasho kina kwenda kumwagika, akatoa kitambaa chake na kujifuta usoni mwake.

“Je….je…je..je…huja onyesha huyo aliye taka kumua?”

“Mmmm acha niombe tena”

Josephine akafumba macho na kumfanya Magreth kumtazama makamu wa raisi jinsi anavyo pepesa pepesa macho kwani hapo ana hisi kwamba ana kwenda kutajwa yeye. Taratibu Josephine akafumbua macho yake na kumtazama makamu wa raisi.

“Nime onyeshwa muuaji”

“Ni..ni…nani?”

“Kuna daktari mmoja alipanga kumchoma sindano ya sumu raisi Mtenzi ila sijamfahamu kwa jina ila nikimuona basi nina weza kumtambua”

“Kweli!!?”

Makamu wa raisi alizungumza kwa mshangao huku mapigo yake ya moyo kidogo yakitulia taratibu.

“Ndio”

“Basi tuta hakikisha kwamba huyo daktari tuna mpata na ata eleza ni kwa nini alipanga kufanya hivyo. Je una weza kuona ni sehemu gani alipo raisi Mtenzi”

“Ndio nime onyeshwa”

Magreth moyo wake uka mstuka sana huku na akamtazama Josephine ambaye ana tambua kwamba janaga moyo wa kudanganya.

“Ni wapi?”

Makamu wa raisi aliuliza huku akijiweka sawa kwenye kiti chake.

“Yupo mkoani Morogoro, ila sijatambua ni sehemu ani ambayo yupo ila nina onyeshwa yupo katikati ya mashamba ya mpanga”

“Kwa hiyo yupo Morogoro?””

“Ndio ila sifahamu ni eneo gani?”

“Basi nina shukuru sana binti, acha nikatume vijana kuhakikisha wana kwenda kumtafuta. Morogoro ni eneo dogo sana hivyo tuna weza kulipata kwa muda mfupi tu”

“Sawa muheshimiwa”

Makamu wa raisi akaaga na akatoka ndani hapo, akaingia kwenye gari na kushusha pumzi.

“Vipi muheshimiwa?”

“Ilikuwa bado kidogo huyu msichana kunijua. Ila maono yake yame angukia kwa daktari”

“Duu hivi ana ona kweli?”

“Ndio, kwa maana ame juaje kama raisi alitaka kuuwawa. Alijuaje kama kuna dokta alipanga kumuu. Huyu binti anacho kifanya ni kitu cha uhakika”

“Duuu sasa tuna fanyaje?”

“Hakikisha kwamba dokta Masangi ana patikana kabla ya hili jambo halijakwenda vizuri na ameniambia kwamba raisi yupo mkoni Morogoro. Hivyo nina hitaji kuwasiliana na mkuu wa mkoa wa Morogoro aweze kuhakikisha ana tuma vijana kwenye kila sehemu yenye mashamba mkoni hapo ili kuhakikisha raisi ana patikana”

“Sawa mkuu”

Msafara huo ukaondoka nyumbani hapo kwa Magreth na kumfanya kupata amani kidogo. Akafunga geti lake kwa ndani na kurudi sebleni na kumkuta Josephine akiwa katika wasiwasi.

“Ita kuwjae akaenda Morogoro na akashindwa kumkuta?”

“Shauri yao. Kwanza ni muuaji, hapa nilipo kuwa nina mtazama kwenye macho yake niliweza kuona kabisa ana wasiwasi”

“Mmmm yaani nime ogopa sana bado nusu tu nimtaje yeye mwenyewe kwamba ndio muuaji”

“Duu. Ila ume tumia njia nzuri. Ila ina bidi kuimarisha ulinzi kwa raisi la sivyo hawa watu wana weza kurudi”

“Ni kweli je kuna mtu gani ambaye yupo serikalini una muamini?”

Magreth akashusha pumzi huku akimtazama Josephine, akatoa simu mfukoni mwake na kumpigia RPC Karata.

“Magreth habari yako”

“Salama kaka yangu upo wapo?”

“Nime rudi Dar es Salaam si una jua hali iliyo tokea”

“Sawa nina weza kukuona au ukaja nyumbani kwangu”

“Kuna tatizo?”

“Kuna jambo muhimu sana?”

“Ndio kuna jambo muhimu kaka yangu”

“Basi nina kuja si hapo Kigamboni?”

“Ndio”

“Basi dakika ishirini nita kuwa hapo kwa maana nipo kwenye patroo”

“Sawa kaka”

Magreth akakata simu, honi ya gari lake mlangoni ikamfanya atoke, akachungulia nje na kumuona Juma. Akafungua geti kubwa na akaingiza gari hilo ndani.

“Aisee barabara ina lete shinda sana”

“Pole hata sisi wenyewe tume ona. Ila gari halija leta shida?”

“Hii mashine boss sijapata shida yoyote njiani”

“Sawa”

Magreth akashusha mizogo yao na kuingiza ndani kwake. Josephine akagonga mlangoni mwa chumba alichopo dokta Masawe.

“Ni mimi”

Josephine alizungumza mara baada ya kuona dokta Masawe ana chelewa kufungua mlango huo. Taratibu Mlango wa chumba hicho ukafunguliwa.

“Vipi wame ondoka?”

“Ndio”

Dokta Masawe akashusha pumzi taratibu huku akiwa amejawa na wasiwasi mkubwa sana. Dokta Masawe akatoka hadi sebleni na kuchungulia akamkuta Juma.

“Huyu ni nani?”

Dokta Masawe aliuliza huku akiwa amejwa na wasiwsi mkubwa snaa moyoni mwake.

“Huyu kijana wangu. Tafadhali nina kuomba usiwe na mashaka naye. Alafu Juma kun……..”

Magreth kabla ya kumalizia sentensi yake, akasikia honi mlangoni na akatoa na kwenda kufungua geti. Akamkuta RPC Karata akiwa ameongozana na vijana wake wanne.

“Muna weza kunisubiria”

“Sawa mkuu”

RPC Karataa akaongozana na Magreth na wakaingia ndani. Dokta Masawe akastuka mara baada ya kumuona RPC Karaka kwani wana fahamiana.

“Masawe ndugu yangu upo?”

“Nipo kaka”

“Kumbe una fahamiana na mdogo wangu”

“Ndio ndio”

“Kaka nime kuita hapa kwa jambo moja. Ila nina hitaji kufahamu mume fikia wapi katika kumtafuta raisi?”

“Bado ngoma droo. Hali ime kua sio hali ndani ya nchi”

“Je mume weza kufahamu sababu za yeye kutoweka?”

“Hapana, sijafahamu bado ila si unatambua kwamba nina fwata amri ya wakubwa wangu na wala hupaswi kuuliza sana”

“Sawa kaka yangu, kati ya binadamu ambao nina waamini naamini kwamba una tambua wewe ni mmoja wapo”

“Nashukuru kwa hilo Magreth.”

“Huyu ni dokta Masawe kama mulivyo fahamiana. Pia ni ndio daktaria anaye itazama afya ya raisi Mtenzi”

“Ana itazama kivipi?”

“Mimi ndio mtu niliye mtorosha raisi Mtenzi hospitalini.”

“Wewe!!?”

RPC Karata alizungumza kwa mshangao.

“Ndio”

“Wewe ndio ume wapiga wale wanajeshi?”

“Ndio na raisi yopo hapa”

“Kwa nini sasa ume mtorosha”

“Makamu wa raisi lisaa moja alikuwepo hapa. Ishu yake ilikuwa ni kuuliza ni wapi alipo raisi Mtenzi”

“Ana wauliza nyinyi kwa nini?”

“Ndugu yangu hapa Josephine ana uwezow a kuona maono ya sehemu alipo mtu yoyote anaye mkusudia na huyu ndio alitoa ripoti ya swala la milipuko inayo endelea na pia ndio alionyesha raisi sehemu alipo fukiwa.”

“Ahaa sasa hapo nime waelewa. Ehee kwa hiyo mume mueleza makamu wa riais kwamba raisi mupo naye?

“Hapana”

“Kwa nini sasa?”

“Kwa maana raisi yeye ndio ana husika katuka kutka kuyaondoa maisha ya raisi Mtenzi”

“NINI?”

“Ndio, ana husika na alimuagiza dokta Masawe ili amuue raisi Mtenzi na baada ya jaribio kushindikana, makamu wa raisi akatuma mlinzi wake ili kumua dokta Masawe”

“Mungu wangu, hii nchi sasa ina elekea wapi?”

“Ndio hivyo kaka yangu. Hapa ninavyo zungumza, Josephine ame wadanganya kwamba raisi Mtenzi yupo mkoani Morogoro na usishangae ikatolewa amri ya askari kuelekea mkoa wa Morogoro kumtafuta raisi Mtenzi”

RPC Karata akashusha pumzi kwani hayo anayo yasikia na jinsi anavyo mfahamu makamu wa raisi bwana Madenge Jr ni mtu mwema na ambaye hana matatizo na viongozi wa chini yake.

“Raisi yupo wapi?”

Magreth akatangulia na RPC Karata akamfwata kwa nyuma. Wakaingia katika chumba hicho na RPC Karata hakuamini kumuona raisi Mtenzi sehemu huyo. RPC Karata machozi yakaanza kumlenga lenga na kumfanya Magreth kujawa na mshangao kwani hajui ni kwa nini RPC Karata ametawaliwa na huzuni kubwa kama hiyo ikiwa yeye ni askari mkakamavu.



“Huyu mzee kipindi nilipo kuwa depo alinilelea kama kijana wake. Alinipenda sana kwa maana nilikuwa mchapakazi na pia alinipa kazi ambayo kusema kweli haiwezi kufutika kwenye ufahamu wangu wa akili”

“Kazi gani?”

Magreth alizungumza kwa sauti ya upole huku akimtazama RPC Karata usoni mwake.

“Mwanaye wa kwanza alikuwa ni jambazi katika mkoa wa Kagera. Alijihusisha na maswala ya utekaji wa magari na mambo mengi sana ya kihalifu. Kipindi hicho muheshimiwa alikuwa ni RPC Katika mkoa huo wa Kagera. Alinipa kazi ya kumuua mwanaye na genge lake hivyo nilijitahidi kadri ya uwezo wangu kuhakikisha nina lisambaratisha genge hilo na niliweza kufanikiwa”

“Duu kwa hiyo alijua kabisa kwamba una muua mwanaye?”

“Ndio, hapakuwa aliye amini kama muheshimiwa atatoa ruhusa hiyo. Isitoshe ana watoto wawili tu wa kiume mmoja ni yule niliye muua na mwengine ni huyu Jery ambaye kwa kipindi hicho alikuwa bado mdogo sana”

“Ahaa kwa hiyo Jery na kaka yake walipishana kwa miaka mingi?”

“Yaa walipishana miaka mingi. Baada ya hapo mimi ndio nikawa mwanaye wa hiyari na nina muheshimu kama baba yangu hadi leo”

RPC Karata alizungumza huku akijifuta machozi usoni mwake.

“Una uhakika kwamba makamu wa raisi alihitaji kumuua raisi?”

“Ndio na Josephine ndio aliye weza kuliona jambo hilo na baada ya hapo tuka fanya jitihada za kwenda kumuokoa katika hospitali ya Muhimbili. Sikuwa na jinsi zaidi ya kuhakikisha kwamba ina pambana na wale wanajeshi na nilifanikiwa kumtoa raisi pale hospitalini. Endapo tunge chelewa kutekeleza jambo hilo basi nina uhakika wa asilimia mia moja sasa hivi raisi ange kuwa maiti kwani dokta Masanja ame kiri kabisa kwamba yeye ndio alipewa dili hilo la kumuua raisi Mtenzi.”

“Masawe huyu?”

“Ndio yeye ndio alipewa jukumu la kumuua raisi Mtenzi tena kwa kumchoma sindano ya sumu”

RPC Karata macho yakamtoka. Akachomoa bastola yake kiunoni na kutoka chumbani hapo huku akiwa amejawa na hasira kali sana. Akatoka chumbani hapo na breki ya kwanza kufika sebleni, akamkwida dokta Masawe shati lake maeneo ya kifuani huku bastola yake akiwa ameiweka chini ya kidevu ya dokta huyo. Juma na Josepgine macho yakawatoka huku wakiwa hawaelewi ni kwa nini RPC Karata ana amuua kufanya hivyo kwa mtu ambaye walikuwa wana changamkiana dakika chache zilizo pita.

“Niambie ni kwa nini ulihitaji kumuua raisi?”

Dokta Masawe mwili mzima ukaanza kumetetemka haja ndogo akashindwa kuizuia na kujikuta akilowanisha suruali yake. Magreth hakuhitaji kuingilia ugomvi huo na zaidi alihitaji RPC Karata aweze kusika ukweli wa jambo hilo.

“Ni…n…ni…m….a..ka..mu wa…raisi alinipa kazi..ya kumuua”

“Alikuahidi kukupatia nini?”

“Mi..li…oni mi…a na kuni…pandi.sha cheo”

Dokta Masawe alizungumza kwa sauti iliyo jaa kigugumiza sana.

“Ulikula kiapo hichi ndio ulicho kiamua kukifanya. Milioni mia moja na cheo kwa uhai wa kiongozi mkubwa wa nchi. Raisi eheee?”

RCP Karata aliendelea kufoka na dokta Masawe akakosa majibu.

“Watu kama nyinyi hamstahili kuishi kabisa”

RPC Karata alizungumza na kumsukumia dokta Masawe kwenye sofa akakoki bastola yake kwa kuziruhusu risasi ziwete kutoka.

“NAOMBA UNISAMEHEE NDUGU YANGU NIPO TAYARI KUMUHUDUMIA RAISI HADI APONE. NAOMBA NAFASI NYINGINE”

Dokta Masawe alizungumza huku akiwa amepiga magoti chini na kuvifumbata viganja vyake kwa pamoja huku akilia kwa uchungu sa kujutia kwa kutanguliza tama ayake mbele pasipo uzalendo.

“Endapo baba yangu mlezi ata kufa. Basi wewe nawe uta kufa na sinto kuacha. Fala wewe”

RPC Karata mara baada ya kumaliza kuzungumza hivyo akachomoa magazine ya bastola yake na kuirudisha kiunoni huku magazine akiichomeka mfuko wake wa nyuma.

“Nashukuru sana”

Dokta Masawe alizungungumza kwa huzuni kubwa sana hadi Juma na Josephine wakamuonea huruma.

“Mage nina kupa ruhu ya kumuya huyu mpumbavu, endapo ata dhubutu kutoroka, au kumuua raisi. Sawa”

“Sawa kaka”

“Nina ondoka nina endelea na patrol ya mji. Nikiendelea kukaa hapa nina weza kumuua huyu mpumbavu”

“Sawa sawa. Alafu kuna vifa aliagiza dokta Masawe kwa ajili ya kumtibu raisi. Nina omba kama ita wezekana uwende na Josephine Agakhan kuna daktari mmoja dokta Masanja ame agiza muonana neya ata pewa hivyo vifaa. Ukiwepo na wewe nina imani kwamba ita tia uzito sana juu ya upatkikanaji wa vifaa hivyo”

Magreth alizungumza na ushawishi wake ukamfanya RPC Karata kumtazama kwa sekunde kadha akisha kisha akatingisha kichwa akimaanisha kwamba ame kubali.

Josephine na RPC Karata wakaondoka nyumbani hapo na kuelekea hospitali ya Agakhan. Magreth akamtazama dokta Masawe pamoja na mikojo yake iliyo tapakaa kwenye sakafu hiyo. Akaingia chumbani kwake, akatoka na pensi pamoja na tisheti ambazo zilikuwa zina valiwa na Evans kipindi ana ishi naye.

“Bafu lipo hapo. Una weza uka oga”

“Nashukuru”

Dokta Masawe alijibu kwa upole huku aibu ikiwa ime mtawala kisawa sawa. Akaondoka sebleni na Magreth akasafisha sebleni kwake.

“Huyu RPC ana undugu na raisi?”

“Ni baba yake wa hiyari”

“Ahaa ndio maana ame kasirika?”

“Wee acha jamaa likuwa an afumuliwa ubongo leo”

“Yani niliogopa, nilijua banamu banamwagika”

Kauli hiyo ya Juma ikamfanya Magreth kucheka sana.

***

“Nime sikia kwamba una uwezo wa kuona mambo yajayo au yanayo tokea”

RPC Karata alimuuliza Josephine huku akimtazama usoni mwake.

“Ndio”

“Je mke wa raisi Mtenzi yupo wapi kwa sasa?”

“Muhimbili”

“Wodi gani?”

“Mochwari”

RPC Karata akastuka kidogo huku akimkazia macho Magreth.

“Una taka kuniambia kwamba yule mama ame fariki?”

“Ndio ame fariki. Kwenye lile gorofa walio pona ni waty watano Tu. Jery, baba yake, mke wake pamoja na walinzi wawili.

“Tuelekeeni Muhimbili”

RPC Karata alizungumza kwa msisitizo wake na dereva wake akabadilisha muelekeo wa gari.

“Ila imetupasa kuelekea Agakhan”

“Nataka kwenda kuhakikisha kwa macho yangu”

RPC Karata alizungumza huku machozi yakimlenga lenga. Wakafika hospitai ya Muhimbili. Ashuka kwenye gari na kuongoza njia ya kueleka katika jengo la kuhifadhia maiti. Josephine hakuitaji kushuka kwenye gari hilo kwamanaa ni muoga sana wa kushuhudia maiti za watu.

“Mwili wa first lady upo wapi?”

RPC Karata alimuuliza mtu anaye shuhulika na kuhifadhi maiti hizo.

“Huku”

Jamaa huyo mwenye rasta zilizo simama na macho yake yaliyo tawaliwa na uwekundu wa kuvuta bangi. Hakujibu chochote zaidi ya kuanza kuingia ndani ya jengo hilo huku akiziruka ruka maiti za watu walio fariki katika mashambulizi ya mlipuko. Akafungua moja ya friji kubwa na akavuta moja ya droo ya friji hilo.

“Huyu hapa”

RPC Karata macho yakamtoka, hakumuamini mwana mama ambaye amejaliwa kuwa na roho nzuri na mwenye kumcha Mungu leo hii yupo kwenye sanduku hilo la kuhifadhia maiti.

“Mwili wake ume dhibitishwa na dokta kwamba ame kufa?”

RPC Karata alizungumza huku akiwa amejawa na mchozi hata swali hilo alilo liuliza hakulitarajia kama ata liuliza hivyo.

“Mzee baba mtu akidanja hakuna haja ya kudhibitishwa na dokta. Mdano huyu mama”

Muhudumu huyo akavuta droo hiyo yoye nje na akafunua shuka eneo la kiunoni, RPC Karata ujasiri wote uka muishia kwani mkewa raisi Mtenzi eneo la kuanzia miguuni mwake lote lime pondeka pondeka vibaya sana. RPC Karata akatoka ndani hapo hauku akiwa na machungu mengi sana. Hata wasaidizi wake waliweza kuligundua hilo kwa haraka na jambo la pekee walilo lifanya ni kumrudisha kwenye gari kwani ana mwagikwa na mchozi mithili ya mtoto mdogo.

***

“Ndio muheshimiwa makamu wa raisi”

“Nime pata habari kutoka kwa mtu ninaye muamini. Watu wana sadikika kwamba wame mtekea raisi Mtenzi kwa sasa wapo mkoa wa Morogoro. Hivyo hakikisheni kwamba muna kwenda kuwasaka mkoa mzima. Ume nielewa RC?”

“Ndio muheshimiwa nime kuelewa”

“Nahitaji hadi kukipambazuka muwe mume nipatia jibu la wapi alipo raisi”

“Sawa”

Makamuwa wa raisi bwana Kadenge Jr akakata simu huku akiwa amejawa na hasira kwani mipango yake ya kumalizia kuamuua raisi Mtenzi ina kwenda kuwa migumu.

“Hawa walio mchukua raisi nikiwapata haki ya Mungu nita waua kwa mkono wangu mimi mwenyewe”

“Ila muheshimia kwa namna moja ama nyinngine wata kuwa wame kupunguzia kazi”

“Kazi kivipi?”

“Hatujio walio mchukua ni watu wa aina gani. Ila kwa asilimia kubwa nina hisi kwamba ni watu ambao ni wabaya na walio kuwa na mpango wa kumuua raisi kwa bomu. Sasa wame ona kwamba wameshindwa hivyo wame amua kumchukua wao wenyewe wakamlazie”

Mlinzi wa makamu wa raisi alizungumza huku akimtazama mkuu wake.

“Etii ehee?”

“Ndio mkuu, hii ishu ni personal na ime garimu maisha ya watu wengi sana. Wewe mwenyewe ume iona ile clip ya Al-Shabab. Wame kiri kuhusika na hili shambulizi kwa sasabu moja tu, walishambuliwa kwenye bandari yao. Nao wameona wamefanya malipizi kwa jiji zima la Dar tena siku ya harusi ya mtoto wa raisi. Hivyo usiumize kichwa kiongozi wangu. Endapo mwezi wa kwanza uta pita, mwezi wa pili uta pita mwenzi wa tatu mkuu una chukua nchi”

Makamu wa raisi akajikuta akitabasamu kwa maana tamaa yake kubwa ni kuhakikisha kwamba ana pata madaraka ya kuwa kiongozi wa juu kabisa kwenye nchi hii ya Tanzania.

“Hapo kidogo ume nifumbua akili yangu”

“Ndio muheshimiwa hatupaswi kutumia nguvu nyinngi sana katika hili swala.”

“Ila hakikisha una mpata dokta Masawe na kumuua”

“Usijali muheshimiwa, nita dili naye. Alafu kuna habari muhimu nime ipata ambayo ita zidi kukupatia wewe nguvu”

“Habari gani?”

“Nime sikia kwamba mke wa raisi naye ame fariki dunia”

“Weee?”

“Ndio, nime ipata habari hiyo kutoka kwa askari mmoja msaidizi wa RPC Karata na ameniambia kwamba wamedhibitisha kabisa kuuona mwili wa mrs Mtenzi”

“Kwa hiyo mke wangu rasmi naye ana kwenda kuwa first lady”

“Ndio muheshimiwa”

Makamu wa raisi akajikuta akichia kicheko cha kejeli kwani malengo yake ya kuiongoza Tanzania hayato kuwa na mpinzani wa aina yoyote.

***

RPC Karata akashuka kwenye gari huku Josephine akiwa ana mfwata kwa nyuma.

“Mkuu”

Josephine aliita na kumfanya RPC Karata kugeuka kusimama na kugeuka kwa nyuma.

“Nina jambo la naomba nikueleze”

“Zungumza”

“Yule kijana wako mrefu na mweusi. Usimuambie kabisa juu ya hili jambo la uwepo wa raisi Mtenzi ndani ya nyumba ya Magreth”

“Kwa nini?”

RPC Karata alizungumza huku akimtazama kijana wake huyo aliye simama eneo la nje kuhakikisha ana endelea kuimarisha ulinzi wa mkubwa wake huyo.

“Ana penyeza siri kwa kila kinacho endelea kwa mlinzi wa makamu wa raisi ambaye ndio alipewa jukumu la kumuua dokta Masawe ili siri yao isivuje. Isitoshe habari ya kufariki kwa mrs Mtenzi amesha ifikisha kwa mlinzi huyo”

“Pumbavu kweli huyu”

RPC Karata akataka kumfwata kijana wake huyo ila Josephine akamshika mkono.

“Nini?”

“Usimkasirikie ila muombe simu yake uta dhibitisha kile ninacho kuambia”

RPC Karaka akashusha pumzi iliyo punguza jazba yake kidogo. Akamuita kijana huyo kwa ishara na akawafwata hadi walipo simama.

“Nipe simu yako, kuna mtu nahitaji kumpigia”

“Sawa muheshimiwa”

Jamaa huyo akatoa simu yake pasipo kufahamua na pelelezwa.

“Ina neno la siri”

RPC Karata alizungumza na kijana huyo akatoa neno hilo la siri kisha akamkabidhi mkuu wake simu hiyo. RPC Karata akajifanya ana ingiza namba huku wakiondoka eneo hilo na Josephine. Wakafika mapokezi na kumuulizia dokta Khan na wakaelekezwa ofisi yake ilipo. RPC Karata akajikuta akisimama huku akisoma meseji za kijana wake ambazo zime mstua sana na kujikuta akichomoa bastola yake taratibu huku hasira ikiendelea kumtafuna moyoni mwake kisawa sawa.



Josephine akwahi kumshika RPC Karata mkono wake kwani kuba baadhi ya watu walisha anaza kumtolea macho huku wakiwa wemejawa na wasiwasi.

“Muheshimiwa hapa ni hospitali watu wana kushangaa”

Josephine alizungumza kwa sauti ya upole na iliyo jaa unyeyekevu mkubwa sana. RPC Karata akamkabidhi Josephine simu hiyo ili aweze kusoma mesji hizo.

‘Bado nina endelea kupeleleza nyendo za RPC’

‘Hakikisha una fahamu kila kitu kinacho endelea kwa maana huyo tuna mjua ni mpambe wa raisi Mtenzi’

‘Ni kweli, je uma niahidi nini kwenye hili’

‘Uta kuwa RPC wewe mara baada ya makamu wa raisi kuchukua nafasi ya uraisi’

‘Sawa je raisi akipatikana’

‘Hawezi patikana na pia ikiwezekana ukipata nafasi muue mkuu wako ili njia yako iwe nyeupe’

Josephine macho yakamtoka. Kitendo cha kunyanyanyua uso wake ili kutazama alipo RPC Karata, hakuweza kumuona.

“Mungu wangu”

Josephine alizungumza na kuanza kukimbilia kuelekea nje. Akamkuta vijana wengine wa RPC Karata wakiwa wame mshikilia kijana huyo huku wakiwa wame mpokonya bunduki yake na wame mfunga pingu.

“Una taka kuniua mimi kwa ajili ya madaraka eheee?”

RPC Karata alizungumza huku akimshushia ngumi ya uso kijana wake huyo aliye wekwa chini ya ulinzi mkali.

“Hapana bosi sijui unacho zungumzia”

RPC Karata kwa haraka aka mkwapua Josephine simu hiyo na kuwaonyesha vijana wengine meseji hizo. Kila aliye soma alijawa na mshangao ime kuwaje rafiki yao ame ingingia kwenye msafara wa mamba ikiwa yeye ni Kenge.

“Muingizeni kweye gari alafu na huyo mpumbavu mwenzako nita hakikisha nina shuhulika naye.”

Vijana hao wa RPC Karata wakatekeleza agizo hilo la bosi wao na wakamuingiza ndani ya gari kijana huyo kisha RPC Karata na Josephine wakaelekea kwenye ofisi ya dokta Khan.

‘Mbona nyinyi ingia bila bisha hodi’

Dokta Khan alizungumza kwa ukali huku akiwakazia macho RPC Karata na Josephine walio simama mbele yake. RPC Karata hakuzungumza kitu chochote zaidi ya kunyoosha mkono wake kwa Josephine ambaye alielewa kusudio la RPC Karata. Akatoa karatasi hiyo aliyo kabidhiwa na dokta Msangi na akamkabidhi RPC Karata ambaye moja kwa moja akaiweka mezani kwa dokta Khan.

“Nahitaji hivi vifaa?”

Dokta Khan akaichukua karatasi hiyo, akaivaa miwani yake na kuangalia kilicho andikwa kwenye karatasi hiyo.

“Mimi siwezi toa vifaa vya hospitali hii peleka kwa hospitali ya serikali pasipo malipo yoyote”

“Dokta Masawe ndio ame tuagiza”

Josephine alijibu.

“Jua vizuri dokta Masawe, ila vifaa hivyo ni very expensive.”

“Kwa hiyo una tupa au hutupi?”

RPC Karata aliuliza kwa sauti ya kukoroma.

“Siwezi toa, lazima tufanye negotiatios ili tujue na sisi tuna nufaika vipi?”

RPC Karata akachomoa bastola yake na akamvuta dokta Khan karibu yake huku bastola hiyo akiwa ameiweka shavuni mwake.

“Una nijua mimi ni nani?”

“Nd..i…i..o”

“Mimi ni nani?”

“RPC”

“Una jua nina shuhulika na watu na waina gani?”

“Wahalifu”

“Sasa usitake na wewe nika kuvisha joho la uhalifu. Nchi ipo kwenye shida, wewe una taka kutuletea maswala ya pesa au una hitaji kesho uka panda ndege na kurudi kwenu India?”

“A..haa…hapana”

“Basi tupatie vifaa vyote vilivyo andikwa hapa tena vikiwa katika ubora mzuri. Umenielwa?”

“Ndi….io muheshimiwa”

Dokta Khan alijibu kwa unyeyekevu uliyo jaa woga mwingi sana kiburi chote alicho kuwa ana kionyesha awali kime potea. Wakatoka ofisini hapo na wakaelekea katika stoo ya kuhifadhia vifaa vya hospitali hiyo. Dokta Khan akaanza kuonyesha vivaa walivyo agizwa. RPC Karata akwaita viajana wake wawili kwa kutumia simu ya upepo. Wakaingia kwneye stoo hiyo na kuanza kutoa vivaa hivyo na kuvipeleka kwenye gari.

“Vita rudishwa lini?”

Dokta Khan aliuliza kwa sauti ya upole sana.

“Sijui”

RPC Karata alijibu kwa ufupi na wakaondoka eneo hilo. Wakaingia kwenye gari na kuianza safar ya kuelekea nyumbani kwa Magreth. Juma akafungua geti na gari hilo likaingia ndani, askari hao wakashusha vifaa hivyo na kuviingiza hadi sebleni.

“Magreth nina kuomba”

RPC Karata akatoka nje na Magreth akamfwata kwa nyuma.

“Hii ni simu ya kijana wangu. Alikuwa ana chati na yule bodyguard wa makamu wa raisi”

RPC Karata alizungumza huku akimpa Magreth simu hiyo. Akaanza kusoma meseji hizo ambazo hata yeye zili mshangaza sana.

“Ana taka kukua kisa cheo?”

“Ndio maanayake”

“Daa sasa yupo wapi kijana mwenyewe”

RPC akafungua mlango wa gari na kumuonyesha kijana huyo aliye kaa siti ya nyuma huku akiwa ameimarishiwa ulinzi na vijana wengine wawili.

“Huyo mpumbavu ndio anaye hitaji kunia”

“Aisee uso wake wala hauonyeshi kama ni muuji”

“Ndio hivyo. Rafiki yako ndio aliye weza kunistua kwenye jambo hilo ndio maana ume ona tume mtia nguvuni”

Magreth akafunga mlango wa gari hilo.

“Hyu ni tamaa tu ndio zime mkamata. Ina bidi abaki chini ya ulinzi. Alafu sisi tudili na huyu mlinzi wa makamu wa raisi kwa maana yeye moja ndio mtu aliye taka kumuua dokta Masawe na pili tuki mkamta basi tuna weza kupata siri nyingi sana kutoka kwa makamu wa raisi ambazo ana mpango wa kuzifanya.”

“Hilo ni wazo zuri. Je tuta mpata vipi?”

“Niachie hiyo kazi mimi. Wewe kadili na kijana wako na mimi nidili na huyu mshenzi ambaye kama ingekuwa sio uwezo nilio nao ange tuu”

“Sawa hilo nina kuachia wewe. Ila nina kuomba sana usi muue hiyo kijana pasipo mimi kuonana naye”

“Sawa kaka”

“Nina imani vifaa hivyo vina hivyo ndio sahihi?”

“Labda nimuulize dokta”

“Muulize kwa maana vifaa vyenyewe tume vipata kwa tabu sana”

Magreth akarudi ndani na kuwakuta dokta Masawe na Juma wakisaidiana katika kuingiza vivaa hivyo kwenye chumba alicho lazwa raisi Mtenzi.

“Vifa ahivyo ndio sahihi?”

“Ndio nina shukuru”

“Poa”

Magreth akatoka nje na kumjibu RPC Karata jibu hilo la dokta Masawe. RPC Karata akaaga na akaondoka nyumbani hapo na vijana wake huku simu ya kijana wake ambaye ni msaliti akiicha mikononi mwa Magreth.

“Jose”

“Bee”

“Kuna hii kazi nime achiwa hapa ya kumpata msaidizi wa makau wa raisi una ona jambo gani mbeleni.”

“Ngoja kwanza nisali”

Josephine akafumba macho yake kwa sekunde kadhaa kisha akayafumbua.

“Nime pewa jambo la tofauti kabisa”

“Jambo gani?”

“Nimeonyeshwa majeshi ya Marekani yana kuja nchini Tanzania. Ila lengo la majshi hayo ni kuingia nchini ni kuchukua hadhina kubwa sana ambayo ipo chini ya ardhi ya posta. Endapo adhina hiyo tukiipata nchi yetu ina kwenda kutajirika na kuwa mara elfu moja na hapa ilipo”

Magreth macho yakamtoka kwa mshangao.

“Mara elfu moja na hapa tulipo?”

“Ndio ni hadhina kubwa sana ambayo ime achwa kwa miaka elfu moja iliyo pita.”

“Ohoo Mungu wangu. Sasa ina kuwaje?”

“Mission iliyopo sasa hivi ni kuhakikisha kwamba Wamarekani hawaipati hadhina hiyo kwani wakiipata, wana kwenda kutajirika mara dufu na wata kuwa na nguvu kubwa sana hapa duniani”

Magreth akajikuta akishusha pumzi kwa maana hakuwa na habari kabisa na najambo hilo. Meseji ikaingia kwenye simu hiyo na akaifungua, kwa bahati nzuri kijana huyo alitoa neno la siri na kuiacha simu yake kubaki kuwa huru pasipo ulinzi wa neno hilo la siri.

‘Oya kijana mume fikia wapi?’

“Jose kuna meseji ime ingia kutoka kwa yule mshenzi”

“Nani?”

“Mlinzi wa makamu wa raisi”

Josephine akaisoma meseji hiyo kisha akamtazama Magreth.

“Huyu mjinga nahitaji kudili naye sasa hivi”

“Basi muambie muonane”

Magreth akaka kimya kwa sekunde kadhaa kisha akaijibu meseji hiyo.

‘Kaka nina habari nyeti tuna weza kuonana usiku huu?’

‘Ina husiana na nini?’

‘Raisi Mtenzi na hii habari nime ipata kutoka kwa RPC. Sasa kaka fanya tukutane’

‘Poa poa. Wapi sasa tuonane’

“Nikutane naye wapi?”

“Sehemu yoyote ambayo una hisi kwamba ni nzuri kwa usiku huu”

Magreth akajifikiria kisha akamuandikia meseji mlinzi huyo wa makamu wa raisi sehemu ya kukutana. Magreth akaingia chumbani kwake na kuvaa mavazi yake ambayo ana yatumia kwenye kazi zake hizo. Akababa silaha zake zote na akatoka ndani hapo. Juma macho yakamtoka mara baada ya kuuona bosi wake akiwa kwenye mavazi hayo.

“Siri yako usimuambie mtu”

Magreth alizungumza na akatoka ndani hapo. Josephine akamfungulia geti na akatoka ndani hapo na pikipiki yake na kuanza kuelekea eneo kuwahi kabla ya mlinzi huyo wa raisi kufika.

***

“Evans amka amka?”

Jini Maimuna alimuasha Evans na taratibu akanyanyuka kitandani huku akiwa amejawa na lepe kubwa la usingizi.

“Vipi ume kuja saa ngapi?”

“Muda wote huwa nipo karibu na wewe. Sasa sikia kuna habari muhimu sana ambayo nina hitaji kukupatia”

“Habari gani?”

“Kuna hadhina kubwa sana ambayo ipo kwenye eneo la Posta. Hadhina hiyo Wamarekani wame panga kuichukua na endapo wakiichukua nchi yao ita kuwa ni tajiri mara dufu”

“Kwa hiyo mimi nifanyaje?”

“Nahitaji hadhina hiyo ibaki ndani ya nchi hiyo na endapo uta fanikiwa kumuonyesha Makamu wa raisi ni wapi hadhina hiyo ina patikana basi uta fanikiwa kuwa tajiri mkubwa sana duniani kwa maana na wewe uta pata kiasi chako chochote ukitakocho”

Evans akaka vizuri kitandani, huku uchu wa utajiri ukimtawala.

“Una sema nita kuwa tajiri mkubwa duniani?”

“Ndio tena una weza kuwa tajiri hata namba moja duniani na utajiri wako hauto kwisha kabisa, na vizazi vyako zaidi ya saba vina weza kufurahia utajiri huo”

“Duu sasa niambie nini nifanye”

“Nahitaji asubuhi uanze safari ya kuelekea jijini Dar es Salaam. Moja kwa moja uende hadi Ikulu na ukakutane na makamu wa raisi na endapo uta kutana naye basi uta mueleza juu ya hiyo habari”

“Hato nisaliti?”

“Hawezi kukusaliti kwa manaa mimi nita kuwa nyuma yako.”

Evans akatazama saa ya kwenye simu yake na kukuta ni saa nane na dakika ishirini usiku.

“Naweza kuianza safari hii usiku huu huhu. Asubuhi niwe mimesha timba ikulu pale au una onaje?”

“Hakuna shaka ila jambo ni moja. Moja kubwa na gumu sana”

“Jambo gani”

“Ili hadhina hiyo iweze kupatina ni lazima kupatikane mwanamke mwenye maono makubwa sana na damu yake ndio ina weza kufungua mlango wa kuelekea eneo ilipo hadhina hiyo”

“Sasa huyo mwana mke tuna mpatia wapi?”

“Tanzania mwanamke huyo yupo mmoja tu na endapo akifa basi mwanamke mwengine ambaye ana weza kutokea na kuwa na uwezo kama yeye ni baada ya miaka mia moja. Nina imani miaka hiyo mia moja utakuwa umesha kufa ila mimi nita kuwepo hai”

“Niambie sasa huyo mwanamke ana patikana wapi ili hata kwa kumpatia pesa ina bidi tumrubuni na awe upande wetu. Hadhina hiyo ni utajiri una jua”

“Ndio, ila mwanamke huyo ni ngumu sana kwa mimi kumsogelea kwa manaa ana uwezo mkubwa kuliko mimi japo yeye ni bina damu”

“Mmmmm”

“Ndio endapo ange kuwa hana uwezo wa kunishinda basi ninge mchukua kirahisi”

“Niambie ni nani kwa maana kama ni pesa ina weza kutumika na nika mpata kirahisi”

“Ana itwa Josephine ni rafiki wa karibu sana na Magreth na msichana huyu tulikutana naye ile siku pale barabarani tulipo kutana na Magreth.”

Evans akastuka kidogo.

“Yule demu aliye kuwa naa mlazimisha Magreth waondoke?”

“Yap. Yule ndio ufunguo wa hadhina hiyo. Bila yeye, hata Wamarekani wenyewe hawawezi kupata hata jiwe moja la dhababu”

Jini Maimuna alizungumza kwa sauti ya upole na kumfanya Evans kushusha pumzi huku akitafakari ni jinsi gani anavyo weza kumpata Josephine ili wawe wa kwanza kupata hadhina hiyo.



“Njia rahisi ninayo hisi kwamba ita tusaidia ni kuwa karibu na Magreth”

“Alafu?”

“Nita weza kuweka ukaribu na Josephine na nita weza kumchukua na kumpeleka eneo hilo la hadhina”

“Jambo hili halipaswi kuchukua zaidi ya wiki kwa maana jeshi la Marekani lina kuja Dar es Salaam kwa ajili ya ujenzi wa jiji hilo. Hivyo macho yao yatakuwa yana angalia sana eneo la Posta.

Evans akajikuta akikuna kicha chake kwa maana dili hili kwa kweli ni kubwa na yeye ana hitaji utajiri kwa namna yoyote ile.

“Poa acha kwanza nionane na makamu wa raisi kisha tuta jua nini cha kufanya. Huyo demu hata kwa kumteka tuna weza kufanya hivyo”

Jini Maimuna akajikuta akitabasamu.

“Nini?”

“Hivi una mjua Magreth vizuri?”

“Ndio, ni muuza maandazi ambaye nili msaidia kuto bwakwa na vibaka”

“Uliwahi kujitokeza ile siku ila endapo usinge jitokeza wale vibaka wange pata tabu sana.”

“Sija kuelewa”

“Uta elewa ukikibaliana na makamo wako wa raisi katika dili hilo. Safari njema”

Jini Maimuna akapotea na kumfanya Evans kuanza kuanza kujiandaa haraka haraka. Akabeba kila kilicho chake, na kutoka ndani ya chumba hicho. Akakabishisha funguo mapokezi akaingia kwenye gari lake na kuondoka eneo hilo na kuianza safari ya kuelekea jijini Dar es Salaam.

***

Magreth akafika katika eneo alilo kubaliana na mlinzi wa makamu wa raisi. Akasimamisha pikipiki yake eneo ambalo sio rahisi kwa mtu mwengine kuiona, isitoshe giza lililopo eneo hili. Lilisaidia sana pikipiki hiyo kuto onekana kwa urahisi. Baada ya dakika ishirini, gari aina ya Range rover vorge ika fika eneo hilo ila ika simama eneo la mbali kidogo kutoka sehemu alipo jificha Magreth.

‘Njoo kwenye gari’

Meseji hiyo ikamfanya Magreth kushusha pumzi kidogo kwa maana alitarajia kwamba mtu huyo atakapo vika sehemu hiyo ata shuka. Magreth akatoa silaha ndogo vilivyo kaa katika muundo wa nyota. Akaanza kuvizurusha kwenye tairi za gari hilo jambo lililo mfanya mlinzi huyo wa makamu wa raisi ajulikaney kwa jina la Boko kustushwa sana.

Boko akaiandaa bastola yake vizuri, huku akizima taa za gari hilo kwa maana kuendelea kuziwasha ni kuma nafasi adui kuweza kumuona eneo alipo. Kuzima kwa taa za gari hizo, ikawa ni nafasi nzuri sana kwa Magreth kulikimbilia gari hilo. Akavunja kioo cha nyuma kwa kutumia mpini wa upanga wake ulio tengenezwa kwa chuma. Boko akaanza kufyatua risasi nyuma ya gari lake huku akiwa amejawa na wasiwasi mkubwa sana. Gafla akastukukia kioo cha upande wake kikivunjwa. Kabla hajafanya chochote akastukia akipigwa ngumi ya kichwa na kumfanya aweweseka. Magreth kwa haraka akafungua mlango wa gari hili na akamchomoa Boko na kumpiga kigoti cha kifuani na akamuangusha chini. Boko akajaribu kujitutumua ila akajikuta akipikoe kipigo kitakatifu kilicho na ndani ya dakika mbili akawa hajiwezi kabi. Magreth akawasha tochi ya simu ya kijana wa RPC Karata,akamulika ndani ya gari hilo na akachukua simu mbili zilizomo ndani hapo. Akazima tocho hiyo na akamaburuza Boko hadi ilipo pikipiki yake.

‘Nambebeje huyu mjinga?’

Magretg aliwaza huku akimtazama Boko aliye tebwereka mithili ya embe bonyoa. Magreth akatoa simu yake mfukono na kumpigia RPC Karata.

“Ndio”

“Nime mpata na nina kuhitaji”

Magreth akamtajia RPC Karata eneo alipo na hazikupita dakika ishirini. RPC Karata akafika eneo hilo huku akiwa peke yake.

“Ni wewe?”

RPC Karata alimuuliza Magreth aliye valia nguo zilizo ificha hadi sura yake.

“Yap. Mtu wako ukihitaji kumuhoji ni wewe”

RPC Karata akachuchumaa na kumtazama Boko.

“Tumpeleke ufukweni ata zungumza vizuri”

“Sawa”

RPC Karata akamuingiza Boko ndani ya gari hilo na kuanza kuondoka. Magreth akapanda kwenye pikipiki yake na kuanza kuwafwata kwa nyuma. Wakafika kwenye fukwe ambayo haitumiki, wakamshusha Boko na jambo zuri linalo wasaidia ni mwanga wa mbalamwezi unao angaza sana eneo hilo.

“Hee hee”

RPC Karata alizungumza huku akimuamsha Boko.

“Nina imani kwmaba una nijua si ndio?”

Boko akamtazama kwa sekunde kadha kisha akatingisha kichwa akimaanisha kwamba ana amfahamu.

“Kwa nini mume hitaji kumuua raisi Mtenzi”

Boko akastuka sana kwa maana aliamini siri hiyo ipo kwa watu watatu. Yeye, dokta Masawe na makamu wa raisi amabaye ndio ame panga yote hayo.

“Sijui una zungumzia nini?”

“Ana kuchukulisha muda wako”

Magreth alizungumza huku akichomoa kisu kifefu kidogo akamchoma Boko kisu hicho kwenye paja la mguu wa kulia na kumfanya alia kwa uchungu sana.

“Kwa nini ulihitaji kumuua raisi Mtenzi?”

Magreth alilirudia swali hilo huku akiwa amejawa na hasira kali sana.

“Ni makamu wa raisi ndio amepanga kumuua kwa manaa naa hitaji kiti cha uraisi”

Mazungumzo yote hayo anayo yazungumza Boko, RPC Karata aliyarekodi ikiwa ni ushahidi ambao baadaye ana weza kuutumia kwa ajili ya kumstaki makamu wa raisi.

“Kwa hiyo makamu wa raisi ndio ame husika”

“Ndio yeye ndio amehusika kwa asilimia mia moja, mimi ni msaidizi wake tu na nina fwata amri yake tu”

Boko alizungumza huku akilia sana kwani maumivu anayo tapata ka kwenye paja lake hilo sio ya mchezo. Magreth akamtazama RPC Karata, ana RPC Karaka akanyoosha dole gumba la mkono wake wa kulia, taratibu akageuzia kidole gumba hicho chini, ikiwa ni ishara ya kumpa ruhusa Magreth kumuua Boko.

Magreth akachomoa upanga wake huo mrefu na kuikata shingo shingo ya Boko na akatengenisha mwili na kiwili wili chake.

“Nime rekodi mazungumzo haya. Nina imani kwamba mazunumzo haya yatamuingiza makamu wa raisi kifungoni”

“Sawa hakikisha una yatunza na hakikisha una itunza siri yangu ya muonekano huu”

“Usijali kuanzia hivi sasa tuta kuwa tuna shirikiana kwenye kila jambo la usalaama. Nina kuomba uweze kumlinda raisi”

“Sawa. Mimi nina ondoka”

Magretha akaeleke eneo alipo iacha pikipiki yake na akapanda pikipiki yake na kuondoka eneo hilo. RPC Karata akauchukua mwili wa Boko na kuutupia baharini. Akakichukua kichwa cha Boko na kuondoka nacho. RPC Karata akafika katika nyumba kwake. Akatafuta boksi, akakiweka kichwa cha Boko kwenye mfuko wa lailoni na kukiingiza kwenye boksi hilo. Akalifunga vizuri boksi hilo mithili ya zawadi, kisha akaandika kwa nje maandishi yanayo someka, ‘ZAWADI KWA MAKAMU WA RAISI’. Akalibeba boksi hilo na kurudi nalo kwenye gari, akafika eneo la karibu na ikulu, akashuka. Akawatazama omba omba walio lala nje ya moja ya duka, akamfwata mmoja na kumuamsha.

“Vipi?”

“Poa”

“Nahitajiji upeleke hili boksi kwenye geti la ikulu”

“Sasa hivi?”

“Ndio kuna elfu kumi hii. Nina kusubiria hapa”

Omba omba huyo pasipo kujali akababe boksi hilo na akakimbia hadi kwenye geti la ikulu. Akaliweka boksi hilo na akaanza kukimbia. Kitendo hicho kikawafanya wanajeshi wanao linda kuanza kumsimamisha kwa kumkemea kwa sauti kali. Ila omba omba huyo hakuhitaji kabisa kusimama. Mwanajeshi mmoja hakufanya makosa akampiga risasi ya mgongo na omba omba huyo akaanguka na akafariki hapo hapo.

Mlio wa risasi uka mstua RPC Karata pamoja na walinzi wengine kwa ikulu. Wakakimbilia getini na kuwakuta wanajeshi hao wakiusogelea mwili wa omba omba huyo.

“Ame kufa”

Mwanajeshi huyo aliye mpiga risasi ombaomba huyo alizungumza mara baad ay kumgeuza upande wa pili kwani alianguka kifudi fudi.

“Hilo boksi lina nini?”

Kiongozi wa wanajeshi hao aliuliza.

“Hatufahamu mkuu, huyu omba omba aliliteka akalitupa hapa na akakimbia. Tulijaribu kumsiihi asimame ila hakudhubutu. Nika mpiga risasi”

“Isije ikawa ni bomu?”

Ndio hivyo muheshimiwa “

“Hembu lifungue”

Mwanajeshi mmoja akalisogelea boksi hilo. Atatoa kisu kidogo mfukoni mwake na kuanza kulichana boksi hilo kwa utaratibu.

“Kuna nini?”

Mkuu huyu aliuliza huku akiwa ame simama mbali kidogo akitamtazama mwanajeshi wake huyo.

“Kuna mfuko mweusi na eneo la nje kume andikwa zawadi kwa makamu wa raisi.

“Hembu fungua huo mfuko”

Mwanajeshi huyo alitii amri ya bosi wake huku akitetemeka mwili mzima na jasho likimwagika usoni mwake. Mwanajeshi huyo akajikuta akirudi nyuma kidogo huku akiwa amejawa na mstuko mkubwa sana.

“Ni nini wewe?”

Mkuu huyo aliuliza huku akimkazia macho kijana wake.

“Ni kichwa mkuu”

“Kichwa cha nini?”

“Binadamu”

Mkuu huyo akawatazama wanajeshi wengine. Akapiga hatua hadi kwenye boksi hilo. Macho yakamtoka kwa maana kichwa hicho ni cha mtu anaye mfahamu kabisa.

“Mungu wangu”

“Mkuu ina bidi muheshimiwa aweze kuona hili kwa maana ime andikwa ni zawadi yake”

“Muheshimiwa ame lala?”

“Sifahamu mkuu”

“Beba hilo biksi unifwate”

Mkuu huyo alimuambia kijana wake huko huku akitanguliak uelekea ndani. Moja kwa moja akaelekea hadi katika chumba cha makamu wa raisi. Akagonga na baada ya muda kidogo akafunguliwa mlango.

“Samahani muheshimiwa kwa kukuamsha muda huu”

“Bila sahamani kuna nini?”

Mkuu huyo akamtazama mwanajeshi huyo aliye baba boksi hilo.

“Una ujasiri mkuu”

“Ndio maana nime kuwa makamu wa raisi. Ninge kuwa sina ujasiri nisinge kuwa sehemu hii”

“Samahani muheshimiwa sizungmzii ujasiri huo”

“Ujasiiri upi una unungumzia”

“Kijana wako hatupo naye tena”

“Kijana wangu nani?”

“Boko”

“Ame patwa na nini?”

Mkuu huyo akampa ishara mwanayeshi wake huyo aliye baba boksi. Akasogea hadi sehemu alipo simama makamu wa raisi, kisha akalifunua na kumuonyesha makamu wa raisi kichwa cha Boko jinsi kilivyo wekwa ndani ya boksi hilo, kitendo kilicho mfanya makamu wa raisi bwana Madenge Jr kanza kutetemekwa mwili mzima kwani ni masaa machache tu ame toka kuachana na Boko, mlinzi wake namba mojana anaye muamini na kumfichia siri zake nyingi ikiwemo ya kutaka kumuua raisi Mtenzi.



“Ni…n…ani…ame kileta?”

Makamu wa raisi aliuliza huku akiwa amejawa na kigugumizi kikali sana.

“Ni omba omba mmoja ndio ame kiletea, mara ya kwanza vijana wangu walihisi ni bomu. Ombaomba yule alikimbia mara baada ya kulitupia boksi getini na akakimbia. Alivyo jaribu kusimamishwa akaendelea kukimbia na vijana wangu walimpiga risasi”

“Kwa hiyo hamjui ni nani ambaye ame husika na kumuua mlinzi wangu”

“Ndio muheshimiwa”

“Kakitunzeni hicho kichwa, kisha nahitaji muutafute mwili wake popote ulipo ili tumzike kwa heshimwa”

“Sawa muheshimiwa”

Makamu wa raisi akarudi chumbani kwake huku machozi ya hasira yakimwagika usoni mwake. Akajikuta akimwaga vitu vilivyopo meza ya kioo na vikavunjika vunjika.

***

Maji ya bomba la mvua taratibu yakaendelea kumwagika Magreth usoni mwake. Kumbumbu ya mauaji aliyo yafanya muda mchache uliyo pita, bado ina endelea kupita kwenye ubongo wake mithil ya mkanda wa video za tape.

‘Mungu wangu nina kuomba unisamehe’

Magreth alizungumza huku akisikilizia maji ya bomba hilo jinsi yanavyo endelea kumwagikia, akiwa ndani ya bafu la chumbani kwake hapo. Akajitazama kwenye kioo kikubwa kilichopo hapo chooni na kujiona jinsi umbo lake lilivyo umbika vizuri. Mazozi anayo yafanya mara kwa mara kidogo yana muomuondoa manyama uzembe. Taratibu Magreth akaanza kujitomasa maziwa yake na kujikuta akipata msisimko mkali sana.

‘Ahaa sitaki kufanya hivi’

Magreth alizungumza kimoyo moyo. Akajipaka sabuni mwili wake wote, akaoga haraka haraka kisha akatoka bafuni hapo. Akamkuta Josephine akiwa amejilaza kitandani.

“Juma yupo wapi?”

“Amenijalaza sebleni”

“Ahaaa sawa”

“Alafu Mage ume lifikiria swala la hadhina ambayo ipo chini ya ardhi ya Posta.”

“Nisiwe muongo rafiki yangu. Sijafikiria chochote, je tuta ipata vipi hiyo hadhina?”

“Ipo kwene mapango yaliyo chini ya ardhi hiyo. Pia eneo hilo ni eneo lenye nguvu kubwa za giza kwa maana watu walio weka hadhina hizo ni wafalme wa zamani sana”

“Wafalme gani?”

“Sifahamu ila ni hadhina ambazo wafalme hao waliziweka kwa nguvu za giza na pia kuna kiumbe kimesha fahamu juu ya hadhini hiyo”

“Kiumbe gani?”

“Una mkunbuka yule mwanamke ambaye tulimkuta na Evans ndani ya gari lake?”

“Ndio”

“Yule dada ni jini”

“Jini!!!?”

Magreth aliuliza kwa mshangao.

“Ndio ni jini na tena ndio anaye muwezesha Evans katika mipango yake ya kutaka kuanzisha kanisa ambalo halito kuwa kanisa la kumtumikia Mungu, bali litakuwa ni kanisa la kumuabudu jini huyo. Katika kanisa hilo watu watakuwa wana pokea miujiza ya kila namna na wata muona Evans kama mtumishi anaye tumiwa na Mungu, kumbe nyuma yake kuna jini”

“Mmmmm”

“Ndio, na jini huyotayari amesha tambua hizo hazini na amesha mueleza Evans. Evans ata shirikiana na makamu wa raisi na wata nihitaji mimi katika kuwafungulia katika eneo hilo”

“Wewe?”

“Ndio. Mimi ndio mwenye nguvu za kufungua eneo hilo kwa kutumia ndamu yangu. Hakuna binadamu yoyote mwenye uwezo wa kufungua eneo hilo”

Maneno ya Josephine yakamshangaza sana Magreth. Akajikuta akishusha pumzi huku akimtazama rafiki yake huyo.

“Ila msaada wako ndio uta weza kunisaidia mimi kuto ingia mikononi mwao. Endapo Evans na makamu wa raisi wata pata hizo mali basi tusahau kuhusiana na raisi Mtenzi kurudi Madarakani kwa maana makamu wa raisi bwana Madenge ata kuwa na nguvu kubwa sana ya kiuchumi na ataweza kuwarubuni wanajeshi kwa kutumia pesa atakazo zipata. Ana weza kuipindua nchi hata kama raisi Mtenzi ata weza kurudi madarakani”

Magreth akashusha pumzi taratibu huku akimtazama Josephine anaye zungumza kwa huzuni kubwa sana.

“Tunapo endea huko mbele tuta pata tabu sana Mage. Wakati ni wa sisi kuhakikisha kwamba tuna zuia hilo jambo”

“Sasa hizo hazini zipo vipi?”

“Ni eneo ambalo lime tengenezwa kwa madini ya kila aina ya madini yote yenye thamani kubwa duniani yapo hapo. Pia jeshi la Marekani ambalo lina kuja nchini Tanzania wiki ijayo pia lita kuja kwa lengo la kuhitaji hayo madini”

“Mungu wangu daa”

“Ndio hivyo ina bidi tujitahidi katika hilo”

“Tupumzike hadi asubuhi alafu tuta jua nini cha kufanya. Sawa”

“Sawa”

Magreth akavaa suruali yepesi ya kulalalia, akajifunga tenge kifuani mwake na kutoka chumbani hapo. Akaelekea katika chumba alicho lazwa raisi Mtenzi. Akamkuta dokta Masawe akiwa tayari amesha muwekea raisi Mtenzi mashine za kumsaidia kupumua pamoja na mashine inayo hesabu mapigo yake ya moyo.

“Ana endeleaje muheshimiwa?”

“Hali yake nina weza kusema kwamba ina endelea vizuri kwa maana nime weza kumpima na kukuta kuna babadiliko na pale alivyo kuwa ameletwa Muhimbili”

“Sawa nahitaji uhakikishe kwamba ana kuwa katika uangalizi mzuri kwa maana ana paswa kurudi kwenye kiti chake haraka iwezeanavyo”

“Sawa sawa”

Magreth akamtazama dokta Masawe usoni mwake kisha akatoka ndani hapo, akamkuta Juma akikoroma sebleni hapo. Akatoka nje na kuhakikisha kwamba ulinzi wa nyumba yake upo vizuri. Alivyo ridhika arudi ndani kwake na kujipumzisha.

***

Asubuhi na mapema Jery akazinduka kutoka katika usingizi huo wa nusu kifo. Akafumbua macho yake na kuangaza eneo hilo na kujikuta akiwa amelala kwenye kitanda na upande wake wa kulia kukiwa na walinzi wa baba yake ambao nao pia wame wekewa mashine za kuwasaidia katika kupumua.

Baada ya dakika kumi akaingia daktari ambaye ana wafwatilia afya zao kwa ukaribu sana. Daktari alipo muona Jery amezinduka kwa haraka akamsogelea.

“Nipo wapi hapa?”

“Upo hospitali ya Muhimbili muheshimiwa”

“Mama na baba yangu wapo wapi?”

Daktara akapata kigugumizi cha kumjibu jibu hilo.

“Kwanza una jisikiaje?”

“Najisikia vizuri. Nahitaji kumuona mama yangu na baba yangu. Pia nahitaji kumuona mke wangu”

“Ngoja nika muangalie mke wako kwa maana yupo hapa hospitalini”

“Sawa”

Daktari Richard akatoka ndani hapo na kuelekea katika wodi aliyo lazwa Mrs Sanga na Julieth ambao afya zao zina endelea vizuri.

“Habari za asubuhi”

“Salama tu”

“Ahaa mkwe wenu ame weza kudinduka na ana kuhitaji bi Josephine”

Josephine mara baada ya kusika hivyo, akashuka kitandani hapo haraka haraka huku akisukumba bomba lenye matairi ambalo lime ning’iniziwa dripu la maji alilo chomwa mkono wake wa kushoto.

“Kuwa makini”

Daktari alizungumza na Julietha akaendelea na harakati ya kuelelekea ICU. Nabii Sanga naye hakuwa nyuma kuelekea katika chumba hicho. Wakaingia ndani ya chumba hicho na Juliet kwa haraka akakumbatiana na Jery huku wakiwa katika hisia kali za kimapenzi.

“Upo salama mke wangu”

“Ndio mume wangu. Wewe je?”

“Nashukuru Mungu, najisikia vizuri”

Taratibu wakaanza kunyaonya ndimi zao.

“Wazazi wangu wapo wapi?”

Swali la Jery likanfanya nabii Sanga kumtazama daktari huyo kwa maana wote wawili wana fahamu ukweli wa jambo lililo tokewa ka raisi Mtenzi.

“Kuna tatizo ambalo lime wapata wazazi wangu?”

Jerya aliuliza huku akiwa amemkazia macho daktari huyo.

“Niambieni kama kuna tatizo lime wapata wazazi wangu?”

Jery alizungumza kwa kufoka na kumfanya Julieth kumtazama.

“Mkwe kuna matatizo yalijitokeza kidogo sio mazuri. Subiri hali yako ikiwa vizuri, nita kuambia”

“No baba mkwe mimi ni mtoto wa kiume. Niambieni ni kitu gani kilicho tokea kwa wazazi wangu”

Jery aliendelea kusisitizia na kumfanya nabii Sanga kuwasogelea kwa ukaribu.

“Baada ya mlipuko ule wa jana. Muliweza kufukuliwa kwenye kifusicha hoteli ile. Baba yako aliweza kupatikana kwa manaa mulikuwa naye nyinyi wawili pamoja na walinzi hawa. Baba yako aliletwa hapa na kwa habati mbaya inavyo sadikika hadi sasa hivi yupo mikononi mwa Al-Shabab kwa maana walivamia hospitalini hapa, wakawapiga walinzi na wakamchukua baba yako. Hadi sasa hivi hakuna anaye fahamu kwamba kama mzee wako yupo hai au amekufa”

“Una taka kuniambia walio sababisha milipuko kwenye harusi yangu ni hao Al-Shabab?”

“Ndio mkwe”

“Wapumbavu hawa nita waaua. Haki ya Mungu nita waua”

Jery alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake.

“Je mama yangu”

“Ahaa muheshimiwa endapo uta lia sana muheshimiwa hali yako ina weza kuwa mbaya zaidi”

Daktari alizungumza huku akimtazama Jery usoni mwake.

“Nijibu mama yangu yupo wapi?”

“Ahaa….a….a”

“Baba mkwe mama yangu yupo wapi?”

Jery alibadilisha swali hilo mara baada ya kumuona daktari ana babaika babaika.

“Mama yako bado sija pata habari zake. Labda hilo jambo umuuliza daktari”

Nabii Sanga alizungumza kitu anacho kifahamu kwa manaa na yeye hafahamu juu ya mrs Mtenzi.

“Dokta usinitumbulie macho niambie mama yangu yupo wapi?”

“Mama yako ame fariki”

Taarifa hiyo ikawastua watu wote ndani hapo. Jery macho yakamtoka huku yakizidi kukolea wekundu utokanao na kulia kwa muda mrefu pamoja na hasira.

“Haiwezekani mama yangua kafariki”

Jery alizungumza hukua kishuka kitandani, akachomoa vitu vyote vilivyo kuwa vime wekwa kifuani mwake.

“Mochwari yenu upo upande gani?”

“Mume wangu tulia kidogo”

Julieth alizungumza huku naye machozi yakimwagika usoni mwake.

“Nahitaji kufahamu mochwari yenu ipo wapi?”

“Kule muheshimiwa”

Daktari alimuonyesha jengo hilo kwa kupitia dirishani. Jery hakujali kama miguuni mwake hana viatu wala ndala. Akaanza kutembea kuelekea nje na kumfanya nabii Sanga naye kumfwata kwa nyuma pamoja an Julieth. Wakakutana na mrs Sanga mlangoni.

“Mkwe vipi?”

Jery akampita mama mkwe wake huyo pasipo kumjibu chochote.

“Hayupo sawa mke wangu”

Nabii Sanga alijibu hukua kimtazama Jery na Julieth wanao elekea mochwari huku wakiwa katika mwendo wa haraka hadi wakamshinda dokta huyo. Wanajeshi nao hawakumuacha Jery kwani bado ana lindwa kama mtoto wa raisi.

“Ana kwenda wapi?”

“Mochwari kumuangalia mama yake”

“Mungu wangu kwani mama yake ame fariki?”

“Ndio”

“Ohooo mume wangu kamzuie. Ana weza kuchanganyikiwa kijana wa watu”

“Hapana kwa sasa yupo kwenye hali mbaya ambayo endapo mtu yoyote ata mzuia ana weza kumfanya chochote na kumbuka mimi ni mkwe wake, sihitaji kuombana naye. Wewe rudi chumbani kwako sawa”

“Sawa”

Nabii Sanga akaanza kukimbilia eneo wanapo elekea Jery.

“Jery Jery, vaa viatu basi”

Julieth alizungumza na mwanajeshi mmoja kamakabidhi Jery viatu na akakivaa. Wakafika katika jengo hilo la kuhifadhia maiti na wakakuta watu wakiendelea kuangua vilio wengine wakiwa wamezia eneo la nje kwa mana matatizo yaliyo tokea yame wagusa wana Dar es Salaam wengine pamoja na Watanzania kwa ujumla.

“Nahiji kumuona mama yangu”

Jery alimuambia muhifadhi maiti huyo ambaye kwa wingi wa maiti alizo zipokea zikiwa katika hali mbaya, zime mfanya kuongeza kiwango chake cha kuvuta bangi kwa siku kwa maana pasipo kufanya hivyo hato weza kabisa kuifanya kazi hiyo. Kijana huyo akaongoza moja kwa moja hadi kwenye friji kubwa lenye makabati mengi ya kuhifadhia maiti.

“Una ujasisi?”

Jama alizungumza huku akitoa moshi mwingi wa bangi hiyo anayo ivuta puani mwake.

“Fungua”

Jamaa akavuta droo hilo. Jery na Julieth wote wakamshuhuda mrs Mtenzi akiwa amelazwa kwenye droo hiyo inayo fuka moshi wa ubaridi mkali unao gandisha maiti hizo ili zisioze.

“Mama yako, kiwili wili chake cha chini kime pondeka vibaya sana. Je una weza kukiona?”

Swali la muhudumiaji huyo likamfanya Jery kukaa kimya huku machozi yakimwagika. Julieth naye machozi ya uchungu na hasira yakaendelea kumwagika kwani mwana mama huyo alikuwa akimpenda sana na kumjali na alimchukulia kama mwanaye wa kumzaa.

***

“Muheshimiwa raisi tume fanikiwa kuupata mwili wa Boko, ume tupwa baharini huku kichwa chake kikiwa kime gawanyishwa na mwili wake”

Ripoti hiyo ikamfanya makamu wa raisi bwana Madenge kusimama wima kutoka kwenye kiti alicho kikali.

“Yupo wapi?”

“Mwili wake upo kwenye gari muheshimiwa”

Makamu wa raisi akaongozana na kijana wake huyo hadi kwenye gari lililo beba mwili wa Boko, ambao una pelekwa hospitali kwa ajili ya kuhifadhiwa. Wakamfunua shuka lake na makamu wa raisi akadhibitisha kwamba ni mwili wa Boko.

“Mpelekeni hospitalini na mumuwekee na kichwa chake”

Makamu wa raisia lizungumza huku machozi yakimwagika kwani kuondoka kwa kijana wake huyo ni pigo kubwa sana kwake.

“Sawa muheshimiwa”

“Nendeni mukaniletee yule msichana anaye onyeshwa mambo yajayo. Nataka aje anitajie ni nania liye muua Boko. Mume nielewa”

“Sawa muheshimiwa”

Agizo hilo la kwenda kuletwa kwa Josephine likatekelezwa na vijana hao ambao kwa haraka wakaingia kwenye gari na kuainza safari ya kuelekea nyumbani kwa Magreth kwa ajili ya kumchukua Josephine.



Gari mbili kutoka ikulu, zilizo jaa wanajeshi zikasimama getini mwa nyumba ya Magreth. Wakashuka wanajeshi sita na kusimama getini hapo. Mmoja wapo akaminya kitufe cha kengele na wakasubiriwa kwa ajili ya kufunguliwa. Magreth kwa haraka akatoa simu yake mfukoni na kutazama video za kamerza zilizo fungwa getini kwake.

“Hawa ni walinzi wa makamu wa raisi”

Magreth alizungumza huku akimatzama Juma na Josephine walio kaa sebleni hapo.

“Wamekuja kufanya nini?”

“Sijajua na sijamuona makamuwa raisi. Juma ingia ndani kwenye chumba cha daktari na hakikisha kwamba dokta Masawe hatoki ndani na wala hamjulikani kama mupo humu ndani”

“Sawa bosi”

Magreth akatoka nje na kufungua geti dogo.

“Habari zenu”

“Salama, tuna muhitaji Josephine ana hitajika ikulu kwa maagizo ya makamu wa raisi”

“Samahani naomba nione vitambulisho vyenu”

Mmoja wa wanajeshi hao akatoa kitambulisho chake na kumkabidhi Magreth akakisoma na umrudishia.

“Kama hamtojali nita kwenda naye ndugu yangu kwa maana siwezi kumuacha muka ondoka naye peke yake”

“Sawa hakuna shaka”

Magreth akafunga geti hilo na kurudi ndani.

“Vipi”

“Tuna elekea ikulu, si upo vizuri?”

“Ndio”

Magreth akaingia katika chumba alichopo Juma.

“Tuna kwenda Ikulu sasa hivi. Hakikisha kwamba dokta na mgonjwa wana kuwa salama”

“Sawa”

“Dokta kumbuka macho yangu yote yana kuangalia wewe, hakikisha mgonjwa ana kuwa salama”

“Sawa muheshimiwa”

Dokta Masawe alijibu kwa unyonge. Magreth na Josephine wakatoka nje na kuingia kwenye moja ya gari la wanajeshi hao na kuainza safari ya kuelekea Ikulu. Wakafika ikulu na moja kwa moja wakapelekewa katika ofisi ya makamu wa raisi.

“Karibuni na samaani kwa kuwakurupusha ila nime waita hapa nina hitaji kujua jambo moja tu”

Makamu wa raisi alizungumza bila hata ya kuwasalimia Magreth na Josephine.

“Jambo gani muheshimiwa?”

Magreth aliuliza.

“Kwanza kaeni”

“Asante”

Magreth na Josephine wakaka kwenye viti hivyo viwili vilivyopo mbele ya meza ya makamu wa raisi.

“Jana usiku kijana wangu au kwa lugha nyingine, mlinzi wangu wa karibu ameuwawa kifo cha kikatili sana. Ame katwa kichwa chake na nikaletewa hapa ikulu kama zawadi yangu”

“Mungu wangu!!”

Magreth alijikuta akistuka kana kwamba hafahamu kilicho tokea.

“Ndio, nina hitaji kufahamu ni nani aliye husika na kifo hicho. Wewe kama mtabiri unaye ona mambo yaliyo jificha nina hitaji uniambie ni nani ambaye eme husika na kifo hicho”

Josephine na Magreth wakatazamana.

“Samahani muheshimiwa, je ukiwaauliza wachunguzi wako wana dai nini?”

“Hadi sasa hivi sija fwatilia juu ya uchunguzi wao ila nina kuhitaji wewe uweze kuniambia ni nani ambaye eme husika”

Josephine akashusha pumzi taratibu kisha akafumba macho yake kwa sekunde kumi na tano kisha akayafumbua.

“Ume ona nini?”

“Kijana wako ame uwawa na Al-Shabab na wata muua kila mmoja ambaye ana hitaji kushikilia kiti cha uraisi. Wamekutumia zawadi hiyo ili kukuonyesha kwamba wana uwezo wa kukusogelea karibu na kukuua hata kama una lindwa na maelfu ya wanajeshi”

Josephine alimuongopea makamu wa raisi na kumfanya ajawe na wasiwasi mkubwa sana hadi akajikuta akisimama kwenye kiti chake.

“Una taka kuniambia ni Al-Shabab?”

“Ndio muheshimiwa siwezi kukuongopea”

“Mungu wangu, sasa niambie nifanye nini?”

“Ufanye nini muheshimiwa?”

“Kwa sas amimi ndio nina ongoza nchi. Sasa ita kuwaje wakiniua na mimi?”

“Najua ni nafasi ngumu sana muheshimiwa. Ila simamia nafasi ambayo Mungu amekuchagua, ukihitaji nafasi nje ya hiyo ambayo Mungu ame kuchagua kifo chako kita kuwa mapema sana na huto fanikiwa kwenye hiyo nafasi unayo ifikiria”

Josephine alizungumza kimafumbo na kumfanya bwana Madenge Jr kukaa tena kwenye kiti chake huku akiishiwa nguvu kabisa.

“Ina maana….kwamba….ahaahaha sawa, je raisi Mtenzi ata rudi?”

“SIku atakayo patikana ndio siku atakayo rudi”

“Si ume sema yupo mkoa wa Morogoro?”

“Ndio yupo mkoa wa Morogoro. Ila ina bidi muhakikishe kwamba muna ongeza jitihada za kumtafuta”

“Sawa nita fanya hivyo. Nina shukuru kwa maono yako”

“Nashukuru nawe pia muheshimiwa.”

Makamu wa raisi akamuita dereva wake na kumuagiza awarudishe Magreth na Josephine nyumbani kwao. Wakiwa kwenye kordo Magreth hakuamini kumuona Evans akiwa ana ana kuja mbele yao huku akiwa ameongozana na wanajeshi wawili. Walipo karibiana Magreth akasimama na kumfanya Josephine pamoja na dereva huyu kusimama.

“Tumekutana huku pia?”

Evans alianza kuzungumza hukua akiwa amejawa na tabasamu pana sana usoni mwake.

“Ndio, ume kuja kufanyaje hapa ikulu?”

“Nime kuja kwa kazi zangu. Naamini hata wewe ume kuja kwa shuhuli zako”

Taratibu Josephine akamsogelea Evans na kusimama karibu kabisa na sikio lake.

“Natambua jini wako Maimuna ame kuagiza uje kuzungumza upuuzi hapa kwa makamu wa raisi. Ila tambua hujui una dili na mambo ya aina gani na endapo uta kwenda ndani hapo na kuzungumzia kuhisiana na hadhina hiyo. Uta kufa mikononi mwangu na huyo jini wako Maimuna hato kuwa na uwezo wa kukusaidia na familia yako pamoja na lile gorofa ulilo jenga kwanu kwa pesa za kijini vita teketea na utamuacha mama yako kwenye hali ya umasikini mara saba ya umasikini walio kuwa nao mara ya wanza. Chaguo ni lako, kufunga bakuli lako au kupoteza kila ulicho nacho sasa”

Josephine alizungumza kwa sauti ya kunong’oneza ambayo ni Evans pekee ndio alikuwa ana isikia. Woga ukamjaa sana Evans, hamu na shahuku yote iliyo mleta ikulu ikampotea. Akawatazama Magreth na Josephine wanao endelea na safari yao ya kuelekea nje huku nyuma yao wakifwata na dereva wa makamu wa raisi.

“Hei twende”

Mlinzi huyo alimsisitizia Evans ambaye muda wote macho yake ame wakodolea Magreth na Josephine hadi wakapotea kwneye upeo wa macho yake. Akaongozana na walinzi hao hadi ofisini kwa makamu wa raisi.

“Mkuu huyu kijana ana itwa Evans ameo omba kuonana na wewe””

“Una nini cha kuzungumza na mimi?”

“Ahaa…muheshimiwa kuna…kuna”

“Kuna kuna kuna nini? Acha kubabaika kama huna cha kuzungumza mtoeni ofisni kwangu bwana akili yangu haipo sawa”

Bwana Madenge Jr alizungumza kwa hasira kali sana huku akiwatazama walinzi wake hao. Evans akamuona jini Maimuna akiwa pembeni yake.

“Muheshimiwa nina imani kwamba una hitaji nafasi hii na una pata wakati mgumu sana wa kujihakikishia kuichukua hii nafasi”

Evans alizunugmza kimafumbo na kumfanya bwana Madenge Jr kustuka kidogo.

“Naomba mutupishe”

Bwana Madenge Jr alizungumza huku taratibu akiishusha hasira yake. Walinzi hao wakatoka ofisini hapo.

“Rudia ulikuwa una sema”

“Natambua kwamba una hitaji nafasi ya uraisi na mpinzani wako ni raisi Mtenzi ambaye hadi sasa hivi hufahamu ni sehemu gani alipo, si ndio?”

“Wewe ni nani?”

“Nina itwa Evans Shika ni mtumishi wa Mungu ambaye nina uwezo wa kuona maono makubwa sana yajayo na hata nikikutazama wewe nina weza kuona kwamba ni kitu gani unacho kiwaza”

Makamu wa raisi akamkazia macho Evans anaye jibaragazua mbele yake.

“Una jua nina waza nini sasa hivi?”

“Ndio?”

“Niambie”

“Uta wezaje kuwashinda Al-Shabab ambao wame kuwa ni kikwazo kikubwa sana cha nafasi yako ya uraisi kwa ni wame muua mlinzi wako na wemekuletea kichwa”

Maneno yote anayo yazungumza Evans yana toka kwa jini Maimuna ambaye hata yeye ameweza kupotezwa katika maono yake na Josephine ambaye ana uwezo wa kuomba chochote kwa Mungu na akajibiwa wakati huo huo.

“Nipe njia ya kupambana nao?”

“Nahiyaji unihakikishie jambo”

“Jambo gani?”

“Uta nipa nafasi kubwa kwneye nchi ya kutengeneza kanisa langu kubwa na vikwazo vyote ambavyo niliwekewa katika uanzilishi wa kanisa langu vina futwa.”

“Vikwazo gani?”

“Moja raisi Mtenzi alihitaji kunia akishirikiana na mwanaye Jery”

“Nikuamini vipi?”

“Nilikuwa na mahusiano ya kimapenzi na Julieth mkwe wa Mtenzi hivyo walihitaji kunia ikuwa ili kuto kuniaona duniani ili kulinda ndoa hiyo”

Makamu wa raisi akashusha pumzi huku akimtazama Evans usoni mwake.

“Ishu ni wewe kujenga kanisa pekee?”

“Na kulipiza kisasi kwa Jery na Julieth”

“Kwa hiyo una nihakikishia kwamba nita pata kiti cha uraisi?”

“Ndio”

“Kijana mimi sio mtu wa masihara. Endapo sinto pata kiti hichi cha uraisi, nita kuua mimi mwenyewe. Umenielewa?”

“Ndio muheshimiwa”

“Basi ume pata unacho kihitaji. Hao unao hitaji kuwalipizia kisasi kazi ni kwako mimi sinto jihusisha, ume nielewa?”

“Nashukuru muheshimiwa”

“Niambie sasa raisi Mtenzi kwa sasa yupo wapi?”

Jini Maimuna akamnong’oneza Evans masikoni mwake.

“Yupo mkoani Morogoro”

Jibu hilo la Evans likazidi kumfanya makamuwa raisi kumuamini Evans kwani hata utabiri wa kwanza wa Josephine ame mueleza kuhusiana na mkoa wa Morogoro, kitu ambacho ni uongo kwani raisi Mtenzi yupo ndani ya jiji hilo hilo la Dar es Salaam.

***

Magreth na Josephine wakashuka kwenye gari getini kwao na dereva huyo akaondoka zake. Wakaingia ndani huku Josephine akionekana hana furaha kabisa.

“Mbona uso wako una onekana haun furaha?”

“Nahitaji kuingia kwenye vita Mage”

“Vita gani?”

“Vita ya kumuangamiza jini Maimuna. Nimeweza kumdhibiti kwa sasa katika kuona kile ambacho nina kiona mimi. Kwa sasa ana ona yale yote ambayo ni nina zungumza kwa kuganganya na hayo ndio anayo yaona yeye. Kwenye hilo nime fanikiwa ila nahitaji kumrudisha kuzimu kwa maana ana weza kuleta madhara makubwa sana”

“Sasa hiyo vita nita kusaidije?”

“Sio vita ya kuonana na macho Mage. Nina imani kwamba una jua vita za kiroho jinsi zinavyo kuwa”

“Ndio”

“Nahitaji kufunga kwa siku saba kavu”

“Bila kula chochote?”

“Ndio, mbona sio mara moja kufanya hivyo. Nahitaji kuingia kwenye maombi ya nguvu kuhakikisha kwamba nina muondoa kabisa jini Maimuna kwenye huu ulimwengu”

“Sawa sawa”

Baada ya mazungumzo hayo wakaingia ndani. Wakamkuta Juma akiwa sebleni akitazama luninga.

“Vipo ume pata kfingua kinywa?”

“Hapana nina wasubiria nyinyi”

“Vipi mgonjwa hali yake?”

“Kama mulivyo ondoka ipo vile vile, dokta yupo chumbani kwake.”

Josephine akaingia kwenye chumba alicho lazwa raisi Mtenzi. Akamtazama kwa sekunde kadhaa kisha akamsogelea kitandani hapo.

“Maisha ya raisi yapo hatarini dokta. Natambua una jua uwezekano wake wa kupona ni mdogo snaa si ndio”

Dokta Masawe akashusha pumzi taratibu kwa maana ana tambua fika kwamba uwezekano wa raisi Mtenzi kupona ni mdogo sana.

“Ndio”

“Natambua una fanya kazi kwa shinikizo la kuogopa kuuwawa si ndio?”

“Ndio”

“Nahitaji kukaa ndani hapa na raisi kwa wiki moja”

“Sija kuelewa?”

“Najua huja nielewa. Ila kwa matibabu yako hayo ni kwamba lazima raisi ata kufa ndani ya siku mbili zijazo. Nahitaji kumuomba Mungu kumpatia nafasi nyingine aweze kuishi hivyo sitaki ubebe lawama ambayo ita kuepekea wewe kifo. Umenielewa”

“Ndio”

Magreth na Juma wakaingia ndani ya chumba hicho.

“Jose nime sikia vibaya au?”

Magreth aliuliza huku akimtazama Josephine aliye simama pembezoni mwa kitandani alicho lazwa raisi Mtenzi.

“Huja sikia vibaya, huo ndio ukweli. Nina kiona kifo cha raisi Mtenzi ndani ya siku mbili zijazo. Kifo ambacho kita ipelekea nchi katika mateso makubwa sana, zaidi ya haya ambayo tuna yapitia kwani maana makamu wa raisi kwa sasa kinacho muongoza ni tamaa na ata fanya kila liwezekanalo kuipata nafasi ya uraisi”

Magreth na Juma wakajawa na wasiwasi.

“Hichi ninacho kwenda kukifanya sifahamu kama Mungu ata nijibu au laa, ila nime ona kwamba kesho kutwa ata kufa na endapo ata kufa dokta Masawe muta muua pasipo sababu ya msingi hivyo nina waomba kuanza hivi sasa munipe nafasi, nita kaa ndani hapa kwa maombi ya siku saba. Chochote kitakacho tokea nikiwa katikati ya maombi tafadhali musi fanye jambo la aina yoyote. Tume elewana”

“Ndio”

“Ninaomba muniache na mgonjwa sasa”

Josephine alizungumza huku machozi yakimlenga lenga. Magreth, dokta Masawe na Juma wakatoka ndani hapo huku kila mmoja akiwa amejawa na huzuni kubwa kwa maana hawajui ni n ini kitatokea mara baada ya raisi Mtenzi kufariki duniani.


“Dokta ni kweli raisi Mtenzi ata fariki?”

Magreth alimuuliza dokta Msawe kwa sauti ya upole sana.

“Hali yake ilifikia kwa kweli ni mbaya na pia ni hali ambayo kwa hapa ndani na mimi peke yangu siwezi kumuhudumia.”

“Una shaurije?”

“Kwa kuwa Mungu hashindwi na jambo la aina yoyote basi nasi tuendelee kumuomba aweze kupona”

“Sawa”

Kengele ya getini iliyo anza kutia mlio ikamfanya Magreth kutoa simu yake mfukoni mwake na kuangalia ni nani anaye bisha hodi. Akamona RPC Karata akiwa amesimama mlangoni hapo, akatoka nje na kumfungulia.

“Karibu sana kaka”

“Nashukuru, una endeleaje?”

“Nina meshukuru Mungu”

“Karibu ndani?”

“Mimi sio mkaaji sana. Nime pita mara moja kukujuza kwamba kume tolewa taarifa ya kumsaka mtu aliye fanya mauaji ya yule kijana”

“Nina uhakika kwamba hawato weza kufahamu si ndio?”

“Yaa kwa maana mimi ndio nilikipeleka kichwa cha yule kijana ikulu na nina imani kwama muheshimiwa ameweza kuchanganyikiwa”

“Mmmm ume kipeleka vipi?”

“Nilikiweka kwenye boksi na kumpa omba omba mmoja ambaye alikwenda kukitupa katika geti la ikulu, kwa bahati mbaya alipo kuwa ana kimbia alipigwa riasi na akafariki hivyo ushahidi uliweza kufutika”

“Masikini wee”

“Ndio hivyo no way out. Sasa nina hitaji kumfikishia hii audio ya mahojiano na nita mshinikiza aweze kuachia nafasi yake ya umakamu wa raisin a ikiwezekana waziri mkuu aweze kuiongoza nchini”

“Mmmmm ata kuu”

“Najua ata niau ila sinto ipeleka mimi kama mimi. Nitakacho jaribu ni kumtumia kwa mtandoa na hato weza kufahamu ime tokea wapi”

“Sawa ila kuwa makini, wewe si una jua hii hali inavyo endelea”

“Ndio ndio. Vipi hali ya raisi ina maendeleo yoyote?”

“Josephine ameweza kuona kifo cha raisi Mtenzi”

“Nini?”

“Yaa tena ame dai kwamba baada ya siku mbili ana weza kufa. Ila alicho kifanya ni kujifungia chumbani kwa raisi Mtenzi na kumuomba Mungu aweze kumuepushia raisi Mtenzi kifo hicho”

“Dokta Masawe hajafanya upumbavu wake?”

“Hapana haja fanya chochote kwa kweli, ila tumuache Mungu afanye kazi yake kwa maana hata madaktari huwa wana shindwa kuzuia kifo. Nina muamini Josephine ana weza kufanya jambo katika hili”

“Acha nikamuone raisi?”

“Hapana, Josephine emeomba kujifungia ndani hapo ili kuhakikisha kwamba ana yata kuwa maombi ya siku sana bila kula chochote”

“Duu sawa sawa. Acha mimi nika endelee na majukumu mengine”

“Sawa kaka”

RPC Karata akaingia kwenye gari lake na akaondoka na Magreth akarudi ndani.

***

“Nahitaji kuelekea ikulu”

Jery alimwambia mmoja wa walinzi wanao mlinda.

“Ila muheshimiwa bado madaktari hawajakupatia ruhusa?”

“Ndio nina litambua hilo ila nina hitaji kwenda ikulu sasa hivi”

Jery alizungumza kwa msisitizo na mwanajeshi huyo akakubaliana na ombi hilo.

“Nahitaji ubaki hapa nina kwenda ikulu mke wangu”

Jery alimuambia Julieth huku akimtazama usoni mwake.

“Mume wangu haupo sawa. Twende wote”

Jery akamtazama kwa sekunde kadhaa Julieth kisha akamtazama nabii Sanga.

“Muna weza kwenda pamoja mwanangu”

Nabii Sanga alizungumza kwa sauti ya upole huku akimtazama Jery usoni mwake.

“Sawa”

Jery, Julieth na walinzi sita wakaondoka hospitalini hapo na kuelekea ikulu. Ukimya ndani ya gari hilo ukazidi kutawala, taratibu Julieth akamshika mkono Jery.

“Be stronger mume wangu”

“Haya”

Jery alijibu kwa ufupi huku akitazama geti la Ikulu linavyo funguliwa. Gari hizo mbili zika simama na wanajeshi hao wakashuka. Jery akajifikiria kwa sekunde kadhaa kisha wakashuka kwa pamoja na mke wake kwenye gari hilo.Jery akaanza kuongoza njia huku Julieth pamoja na walinzi hao wakimfwata kwa nyuma. Jery na Julieth wakajikuta wakisimama huku wakimtazama Evans anaye kuja mbele yao.

“Ume kuja kufanya nini hapa?”

Jery alimuuliza Evans huku akimshika shati lake.

“Tafadhali una nichafua”

Jibu la Evans alikamfanya Jery amtandike ngumi Evans kichwa cha uso huku akimuachia na kumfanya aweweseke huku akiyumba sana. Jery akataka kumvamia ila walinzi wake wakamzuia kwa ili kuepusha mtafaruku huo.

“Mkamateni mshenzi huyo”

“Hawezi kukamatwa”

Mlinzi ambaye alikuwa akimsindikiza Evans alijibu kwa kujiamini na kumfanya Jery kumshangaa sana.

“Una semaje wewe?”

“Nime sema kwamba hakamatwi na nyote sihitaji mumshike huyu kijana”

“Una zungumza wewe kama nani?”

“Kama mlinzi wa kiongozi wa nchi. Tuna weza kuendelea”

Mlinzi huyo alizungumza huku akimshika mkono Evans na wakaanza kuondoka eno hilo. Evans akamkonyesha Julieth na kumfanya Jery kuzidi kujawa na hasira sana. Evans akapiga hatua kadhaa kisha akasimama, taratibu akarudi sehemu alipo simama Jery na kumsogelea karibu yake.

“Ulinitesa kipindi kile kisa huyo malaya hapo. Ila kwa sasa kibao kimekugeukia wewe hivyo usinitishe”

Maneno hayo ya Evans hayakumpendaza kabisa Jery. Akamvaa Evans na kumuangusha chini akaanza kumshambulia kwa kumpiga ngumi mvululizo. Walinzi wa Jery hawakuhitaji kuamua ugomvi huo kwani Evans ndio aliye rudi na hawajui ni kitu gani alicho kizungumza na kumfanya Jery kukasirika. Mlinzi wa makamu wa raisi akataka kuamua ugomvi huo ila walinzi wa Jery wote wakamnyooshea bunduki zao.

“Usiwaguse”

Walinzi wengine wanao fanya kazi chini ya makamu wa raisi wakafika eneo hilo na kila mmoja akaanza kuwanyooshea bunduki walinzi wa Jery. Julieth akatamani kuamua ugomvi huo ila akajikuta akishindwa kwani kiuhalisia Evans ndio mwanaume wake wa kwanza kumtoa usichana wake. Evans hakuhitaji kuwa mnyonge, akamgeuza Jery na kumuweka chini, akaanza kumshindilia ngumi mfululizo.

“Ni nini kinacho endelea hapo?”

Makamu wa raisi alizungumza kwa kufoka huku akitembea kwa haraka eneo hilo la ugomvi.

“Waamueni”

Hapakuwa na mlinzi aliye weza kupinga amri hiyo ya makamu wa raisi. Wakaachanisha Jery na Evans ambao kila mmoja ana mwagikwa na damu puani mwake.

“Nitakuu wewe mwana haramu?”

Jery aliendelea kufoka huku akijitahidi kujitoa mikononi mwa walinzi wake.

“Jaribu uone, mimi sio Evans yule mnyonge wa kipindi kile nita kuua na wewe”

“Muondoeeni huyo”

Makamu wa raisi alizungumza na Evans akatolewa nje kabisa ya jengo la ikulu. Gari lake likatolewa na akaamrishwa aondoke eneo hilo.

“Daktari aletwe na mpelekeani Jery ndani kwao”

“Sawa mkuu”

Jery akapelekwa katika nyumba wanayo ishi.

“Nita muua yule mshenzi”

Jery aliendelea kufoka huku damu zikimwagika puani mwake. Julieth akachukua moja ya kitambaa na akaanza kufuta Julieth damu hiyo inayo mwagika. Daktari akaingia ndani hapo na akaanza kumpatia huduma Jery ambaye bado ana fura kwa hasira.

“Mume wangu tuliza hasira najua ni jinsi gani tuta dili naye yule mshenzi”

“Lazima nimuue”

Jery aliendelea kulalama. Akaingia makamu wa raisi na kukaa kwenye moja ya sofa.

“Jery mwanangu mbona una kuwa mgomvi kiasi hicho?”

Bwana Madenge Jery alizungumza huku akimtazama Jery usoni mwake.

“Yule ni mshenzi sana”

“Ame faya kosa gani?”

Jery akamtazama Julieth kwa sekunde kadhaa.

“Baba mdogo hayo achana naye. Mume fikia wapi kumpata baba yangu?”

“Bado tuna endelea kumtafuta na wana jeshi wana fanya msako kwenye mkoa wa Morogoro.”

“Kwani ndipo alipo pelekwa?”

“Ndio”

“Ume fahamu kama mama yangu ame fariki?”

“Ndio nina fahamu”

“Nahitaji uwaue wote walio husika kwenye mauaji hayo. Umeinielewa baba mdogo?”

“Nime kuelewa endapo tuta wakamata wahusika basi tuta shuhulika nao kisawa sawa”

“Tukiachana na hayo Evans Shika ame kuja kufanya nini hapa ikulu?”

“Ahaa alikuja kutoa pole”

“Pole kwa nani ikiwa wahusika wa hii ikulu hatupo?”

“Jery kumbuka kwamba raisi anapo kuwa hayupo madarakani mimi ndio nina ichukua nafasi yake”

“Ila na wewe si una ikulu yako kwa nini usiende kuifanyia kazi yako yote kwenye ikulu?”

Jery alizungumza kwa kufoka sana.

“Kumbuka una zungumza na nani Jery. Pia wewe huna mamlaka yoyote kwenye hii nchi, wewe ni mtoto wa raisi na sio raisi. Usilisahau hilo”

“Mume wangu tuliza jazba. Baba mdogo msamehe mume wangu, naamini kwamba hayupo kwenuye wakati mzuri”

“Nina kwenda kuendelea na majukumu yangu. Endapo uta kuwa sana, nipo ofisini”

Makamu wa raisi akatoka ndani hapo.

“Hivi vidonge uta kunywa utakapo jisikia maumivu ya kichwa”

Dokta akamkabidhi vidonge hivyo Julieth kisha akatoka ndani hapo.

“Mume wangu huyu ni baba yako mdogo kweli?”

“Hapana nime zoea kumuita baba mdogo tu. Alafu huyu mzee huwa simuamini sana”

“Humuamini kivipi?”

“Ni mtu mwenye tamaa, ina wezekana ana fahamu ni wapi alipo baba yangu ila ana zingua. Ila ngoja kuna kifaa ambacho ni cha siri sana ambacho ana kifahamu mimi, mama na baba. Kifaa hicho huwa kina muonyesha raisi ni eneo gani alipo”

“Una fahamu kilipo?”

“Ndio nina fahamu ni wapi kilipo”

Jery na Julieth wakaingia katika chumba cha raisi Mtenzi. Jery moja kwa moja akasogeza kitanda, akatoa zulia lililopo chini ya zulia hilo na kukuta mfuniko wa chuma ambao ni mdogo na una batani za kuingiza namba za siri. Jery akaingiza namba za siri na akafungua kimlango hicho. Akakitoa kifaa hicho kilocho kaa kama simu. Akakiwasha, na kikahitaji neneo la siri na akaandika jina la mama mzaa baba yake.

“Hapa sasa ni sawa”

Jery alizungumza huku wote wakikitazama kofaa hicho. Baada ya sekunde kadhaa alama ya kijani ikaonekana.

“Yes baba yupo hai”

“Ume juaje?”

“Endapo ingeonyesha alama nyekundu basi baba angekuwa amesha kufa”

“Weee”

“Ndio na alama inaonyesha baba yupo hapa hapa Dar es Salaam”

“Muambie basi baba yako mdogo ili aweze kutuma jeshi?”

“Hapana tuna kwenda sisi wenyewe”

“Kama watakuwa ni watu wabaya ndio wame mchukua ita kuwaje mume wangu”

“Julieth ninapo kuambia kwamba huyu makamu wa raisi simuamini na kwenye maisha yako sheria namba moja usimuamini mtu yoyote hapa ikulu. Hujui ni sumu ya aina gani ambayo makamu wa raisia me mezeshwa yule mshenzi Evans.”

“Sawa mume wangu”

Jery na Julieth wakaingia katika chumba cha Jery wakabadilisha nguo na Julieth akavaa nguo za Jery ambazo zina mtosha. Wakaondoka eneo hilo la ikulu pasipo walinzi na kuanza kufwata amelekezo ya kifaa hicho sehemu kinapo waelekeza kuelekea.

“Kunja kushoto hapo”

Julieth alizungumza na Jery akakunja kona ya ya barabara inayo inagi kwenye mtaa ambao una majumba mengi ya kifahari.

“Simama simamisha gari”

Julieth alizungumza mara baada ya alama hiyo ya kijani kuanza kucheza cheza kipindi tu walipo fika usawa na nyumba anayo ishi Julieth.



“Alama inaonyesha ni hapa”

Julieth alizungumza na wote wakalitazama geti hilo lililo fungwa.

“Ina kuwaje?”

Julieth alizngumza huku akitazama geti hilo.

“Ina kuwaje kivipi?”

“Hii nyumba ana ishi dada mmoja ana itwa Magreth”

“Una taka kusema yeye ndio ame mteka baba?”

“Sija jua ila ngoja tugonge tuone”

Wakashuka kwenye gari hilo na wakalisogelea geti hilo. Juilieth akaminya kitufe cha kengele walicho kiona kwenye geti hilo. Magreth macho ya mshangao yakamtoka jambo lililo mfanya Juma atambue juu ya mstuko huo.

“Mbona una onekana una wasiwasi?”

“Jery na Julieth wapo hapa?”

“Ndio kina nani?”

“Jery ni mtoto wa raisi Mtenzi na Julieth ni mtoto wa nabii Sanga”

“Wame juaje kama raisi yupo hapa?”

“Kwa kweli sifahamu. Hembu ngoja kwanza?”

Magreth akampigia simu RPC Karata.

“Mage vipi?”

“Jery na Julieth wapo getini kwangu wana gonga je ume weza kuwaleza uwepo wa raisi Mtenzi eneo hili?”

“Hapana, kwani wamesha toka hospitalini?”

“Ndio, sasa sijui ime wame juaje?”

“Hembu wasikilize wana weza wakwa wame kuja labda kuulizia huduma ya Josephine”

“Etii ehe?”

“Yaa kwani wame kuja na walinzi?”

“Hapana nina waona wakiwa wapo wao peke yako”

“Basi wata kuwa wamekuja kumuulizia huyo rafiki yako”

“Basi ngoja niwasikilize”

Magreth akakata simu na kumgeukita dokta Masawe.

“Una weza kwenda jikoni ili wasikukute hapa kwa maana bado hatujui ni nani wa kumuamini”

“Sawa”

Dokta Masawe akaelekea jiko na Magreth akatoka ndani na kufungua geti dogo.

“Habari yako”

Jery alianza kusalimia.

“Salama, niwasaidie nini?”

“Nisikilize Mage, alama ina onyesha kwamba baba yangu mkwe yupo hapa. Tume kuja kiamani na hatujawahulisha askari na endapo tunge wajulisha basi tungekuja na majeshi. Hivyo tuambie kama baba mkwe wangu yupo au hayupo?”

Julieth alizungumza kwa sauti ya msisitizo na iloyo jaa hasira kidogo.

“Una zungumzia nini wewe?”

“Julieth tulia. Dada mimi nina itwa Jery Mtenzi, ni mtoto wa raisi Mtenzi. Nina imani una nifahamu?”

“Yaa nilikuona kwenye tv?”

“Baba yangu aliweza kutoroshwa hospitali ya Muhimbili alipo kuwa amelazwa. Hivyo tafadhali dada yangu, hiki ni kifaa maalumu ambacho kina muonyesha raisi sehemu alipo na kama unavyo ona kina wakia eneo hili kama unavyo kiona.”

Jery alizungumza kwa sauti ya upole huku akimtazama Magreth usoni mwake. Magreth akanyoosha mkono wake na Jery akamkabidhi kifaa. Magreth akatazama alama hiyo jinsi inavyo waka waka na kweli ramani ina onyesha kwamba raisi Mtenzi yupo hapo.

“Ingieni ndani”

Magreth alizungumza huku akimkabidhi Jery kifaa hicho. Wakaingia ndani na akawakaribisha sebleni hapo.

“Kifaa hicho kilikuwa wapi?”

“Ni mali maalumu inayo milikiwa na raisi hivyo watu wake hususani wana familia yake ndio watu wa pekee ambao wana fahamu hilo.”

Magreth akashusha pumzi huku akimtazama Juma ambaye ana yafwatilia mazungumzo hayo vizuri.

“Raisi yupo hapa ila hali yake sio nzuri”

“Una maana gani kuzungumza hivyo kwamba hali yake sio nzuri?”

Jery aliuliza kwa sauti ya upole na iliyo jaa heshima kubwa sana.

“Ajali muliyo ipata ilikuwa ni mbaya sana. Ila jambo ambalo lilikuwa lina kwenda kumtokea lilikuwa ni zaudi ya ubaya”

“Jambo gani?”

“Alipangwa kuuwawa kwa kuchomwa sindano ya sumu akiwa hospitalini kwenye hali hiyo. Ila ndugu yangu aliweza kupata maono juu ya jambo hilo na kitu cha kumshukuru Mungu ni kwamba tulifanikiwa kumuokoa kutoka kwenye tatizo hilo na ndio nika mleta nyumbani hapa”

“Ni nani aliye taka kumuua?”

Julieth aliuliza kwa shahuku ya kuhitaji kufahamu juu ya jambo hilo.

“Makamu wa raisi alihitaji kumuua”

“NINI……!!?”

Jey aliuliza kwa mshangao mkubwa sana.

“Ndio alimpatia tenda mmoja wa madaktari wa Muhimbili katika kutekeleza tukio hilo. Ila kwa bahati mbaya akataka kumuua yule daktari mara baada ya kushindwa kutekeleza jambo hilo.”

“Mke wangu si una kumbuka nilicho kuambia?”

“Ndio mume wangu nina kumbuka”

“Kwa hiyo wewe ndio uliye mtorosha?”

“Mimi na kijana wangu hapa tulishirikiana katika kuifanya kazi hiyo. Maisha ya raisi na uzalendo ni kwanza japo mimi na familia ya mkwe wako hatuna maelewano. Sikutaka kutumia matatizo yangu na familia ya nabii Sanga kumuacha raisi kupata kifo ambacho sio haki yake.”

“Kabla sijamuona baba yangu ila nina kushukuru sana dada Magreth”

Jery alizungumza huku machozi yakimlenga lenga usoni mwake.

“Usijali, dokta Msawe”

Magreth aliita na dokta Msawe akafika sebleni hapo.

“Una weza kuketi dokta”

Dokta Masawe akaketi huku akimtazama Jery usoni mwake.

“Huyu ndio dokta aliye nusurika kifo kutoka mikononi mwa makamu wa raisi”

“Mzee wangu wewe ndio ulipewa jukumu la kumuua baba yangu?”

“Ndio”

“Una uhakika?”

“Asilimia mia moja. Malipo yangu ilikuwa ni milioni mia moja pamoja na kupandishwa cheo. Nilishindwa kutekeleza hili ikiwa wewe nawe ulikuwa ndani ya chumba kile kile pamoja na mke wako na wale walinzi wawili. Nilipo muambia kwamba nime shindwa, akahitaji kunia. Huyo binti ndio aliye nisaidia na kuanzia siku hiyo tuna ishi hapa na muheshimiwa. Huko nje endapo nita utoa uso wangu basi nita uwawa”

Maneno ya dokta Masawe yakamfanya Jery kububujikwa na machozi ya hasira. Unyama ambao ulitendeka kwenye harusi yake makamu wa raisi ana ona hautoshi hadi ana hitaji kumalizia kabisa baba yake.

“Yote aliyefanya ili iweje?”

“Ili apate uraisi”

“Ohoo alishindwa kusubiria baba yangu amalize muda wake na agombanie yeye. Mbona binadamu hatuna shukrani sisi”

Jery alizungumza kwa huzuni kubwa sana huku akiendelea kulia kwa uchungu sana hadi Magreth akamuonea huruma.

“Mama yangu ame kufa, baba yangu hali yake ndio hiyo. Hivi kweli kweli, huyu makaku wa raisi ana paswa kufanya hivi?”

“Usilie mume wangu, jambo la msingi ni kumshukuru Mungu kwamba tume mpata baba”

Julieth alimbembeleza Jery anaye lia kama mtoto mdogo. Kila aliye muona Jery alijikuta akijawa na huzuni kubwa sana.

“Naweza kumuona baba yangu?”

“Ndio ila kwa sasa ana fanyiwa maombi ya siku sana. Ndugu yangu ambaye aliweza kuona jambo hilo kwenye maono pia ame weza kuona kifo cha baba yako baada ya siku mbili ndio maana ame amua kufanya maombi ya mfululizo kwa ajili ya kumuombea baba yako kurudi kwenye uzima.”

“Nionyeshe tu”

Magreth akasimama na kwa ishara akamuomba Jery amfwate. Wakafika kwenye chumba alichopo raisi Mtenzi. Magreth akachukua moja ya stuli na akapanda na kuchungulia kwa kupitia eneo la juu la mlango huo ambalo lina kioo. Akamuona Josephine akiwa amepiga magoti pembeni ya kitanda cha raisi Mtenzi hukua akiomba kwa unyenyekevu mkubwa sana.

“Una weza kumuona kupitia hapa. Muombaji ame omba kuto sumbuliwa hadi siku saba zitakapo kwisha”

Taratibu Jery akapanda na kuchungulia ndani hapo, hakumini kumuona baba yake akiwa amelala kitandani huku mashine za kumsaidia kupumua zikiwa puani mwake. Unyenyekevu ambao ana uonyesha Josephine uka mfanya Jery kuelewa ni kitu gani kinacho endelea kwenye maombi hayo. Jery akaendelea kulia kwa uchungu sana, furaha, amani na upendo ambao alikuwa akionyeshwa na wazazi wake wote ume potea. Julieth uvumilivu uka mshinda, akafika eneo hilo na kumkuta Jery akiwa ana chungulia ndani hapo. Taratibu Jery akashuka na kujikuta akishindwa kuizuia sauti yake ya kulia. Julieth kwa haraka haraka akapanda kwenye stuli hiyo na kuchungulia ndani, akajidhibitishia jambo walilo kuwa wakielezwa na Magreth. Akashuka taatibu huku akiwa mnyonge sana kwani alikuwa ana mchukulia Magreth ni aduia yake mkubwa sana.

Julieth akamshika mkono Jery na wakarudi sebleni wote watatu.

“Mage”

Jery aliita huku akifuta machozi yake.

“Ndio”

“Baba yangu akipona nina kuhakikishia zawadi kubwa sana. Hili ulilo lifanya ni jambo la kishujaa, nina imani kwamba uta kuwa una tafutwa kwa kufanya tukio hilo?”

“Ndio ila hawakunijua. Pia huyo ndugu yangu hapo ndani aliweza kuwaambia eneo ambalo raisi amepelekwa ni mkoani Morogoro “

“Sasa napata picha”

Jery alizungumza huku akimtazama Magrth usoni mwake.

“Picha gani?”

“Makamu wa raisi alituambia kwamba wana jeshi na askari wapo mkoani Morogoro na wana mtafuta raisi”

“Yaa japo hapaswi kundaganya ila ilimpasa kufanya hivyo ili mradi kuhakikisha kwamba maisha ya raisi yanakuwa salama”

“Dada Mage, nina kuamini, nina amini baba yangu yupo mikono salama. Ila siwezi kuendelea kukaa hapa, nahitaji kufanya kitu kwa ajili ya kuhakikisha bwana Madenge ana lipa juu ya hili alilo lifanya kabla ya kwenda kwa hao Al-Shabab walio ua maelfu ya watu ambao hawana hatia”

“Sawa ila Jery kumbuka kwamba endapo uta kuwa ni kikwazo kwa makamu wa raisi basi ana weza kuku. Kuwa makini sana kwenye hilo”

“Usijali dada, kwa kuwa nimesha jua ni adui yangu ni nani basi nita jua ni namba gani ya kutumia uwezo wangu kuhakikisha kwamba nina muondoa makamu wa raisi kwenye hicho kiti anacho kikalia. Ikitokea hata baba yangu ame kufa, ni heri aka patikana kiongozi atakaye ingia madarakani kwa mapenzi ya Mungu kuliko kiongozi atakaye ingia kwa ajili ya tamaa zake yeye mwenyewe”

“Sawa nime kuelewa”

Jery akasimama na akapeana mikono na Magreth, Juma pamoja na dokta Masawe. Julieth naye aka fanya hivyo hivyo kisha wakaondoka nyumbani hapo.

“Bosi hii haitoo leta uhatari wa usalama wetu kwa maana sasa hili jambo sio siri tena?”

Juma alizungumza huku akimtazama huku akiwa amejawa na wasiwasi mkubwa sana.

“Akitoa siri hii basi atakaye kufa ni baba yake. Ila jambo la msingi ni kuhakikisha kwamba tuna mlinda raisi ndani ya hizi siku ambazo Josephine ana fanya maombezi. Akipona sawa asipo pona pia tuta mshukuru Mungu kwa maana kwenye haya maisha hakuna mtu atakaye ishi milele.”

Magreth alizungumza kwa sauti ya upole ambayo dhahiri ina onyesha amejiandaa kukubaliana na kila jambo litakalo kwenda kutokea mbele yake.

***

“Tuna kwenda wapi mume wangu”

Julieth aliuliza huku akimtazama Jery anaye ongeza mwendo kasi wa gari hilo analo liendesha.

“Kwa waziri mkuu”

“Kufanya nini?”

“Yeye ndio mtu ninaye muamini”

“Mume wangu, una tambua ni hali gani inayo endelea. Waziri mkuu naye kwa mafano akikugeuka ita kuwaje ehee?”

Julieth alimuuliza mume wake kwa msisitizo huku akimtazama usoni mwake. Taratibu Jery akapunguza mwendo kasi wa gari hilo na kulisimamisha pembezon mwa barabara. Akaanza kuupiga piga mskani wa gari hilo kwa hasira kali sana, hukua akilia kwa uchungu sana.

“Nita muua kila mmoja aliye husika kwenye hili, haki ya Mungu nita muua”

Jery aliendelea kufoka kwa hasira sana. Julieth akatamani kumueleza Jery juu ya uwezo na nguvu iliyopo nyuma yake ila ana ogopa sana kwa maana chanza cha matatizo haya yote yanayo tokea sasa hivi ni kutokana na vijaa wake kuwaangamiza askari wa baharini na kesi hiyo wakaichonganisha na kundi la kigaidi la Al-Shabab.

‘Ehee Mungu wangu nita fanya nini mimi?’

Julieth alizungumza kimoyo moyo huku akimtazama Jery aliye inamisha kichwa chake kwenye mskani wa gari hilo huku akiendelea kulia kama mtoto mdogo.

“Mume wangu”

“Mmmmm”

“Nina mpango katika hili, je upo tayari tushirikiane?”

Jery taratibu akanyanyua kichwa chake na kumtazama Julieth usoni mwake kisha akatingishwa kichwa akimaanisha kwamba ame kubaliana na chochote atakacho kizungumza mke wake huyo ambaye hawajapata mapumziko ya faragha toka walipo funga ndoa yao kanisani na mapunziko yao yame angukia kwenye matatizo yanayo umiza mioyo yao.



“Makamu wa raisi kwa sasa ndio anaye sikilizwa kwenye serikali nzima. Waziri mkuu tuna weza kumueleza jambo ila akalifunjisha kwa maana na yeye hatuhitaji kumuamini. Ninacho kushauri mume wangu, tukodishe wauaji ambao wana weza kumuua makamu wa raisi na sekeseke lote hilo tuna wapelekea Al-Shabab?”

“Ni nani ambaye ata ifanya kazi hiyo kikamilifu?”

“Nipe hadi jioni alafu tuta jua ni nani ambaye ana weza kuifanya kazi hiyo”

Jery akamtazama Julieth kwa sekunde kadhaa kisha akamkumbatia kwa nguvu.

“Nakupenda mke wangu”

“Nina kupenda pia mke wangu”

“Twende wapi sasa hivi?”

Jery alizungumza huku taratibu wakiachiana.

“Twende nyumbani kwa maana hapa njaa ina niuma sana”

Jery akawasha gari na wakaondoka eneo hilo. Wakafika nyumbani kwa nabii Sanga na kuwakuta wazazi wa Julieth.

“Baba tuna waze kuzungumza”

Julieth alimuambia nabii Sanga mara baada ya kuingia sebleni.

“Ndio”

Wakatoka nje na kumuacha Jery akikaa kwenye sofa huku akiwa mnyonge sana.

“Vipi?”

“Tume fahamu ni sehemu gania mbapo raisi Mtenzi yupo”

“Ni wapi?”

“Huwezi amini baba, yumbo nyumbani kwa yule mshenzi Magreth”

“Mage huyu ninaye mjua mimi au mwengine?”

“Huyu huyu.”

“Haka kasichana ni kashenzi sana, kwa nini sasa alimtorosha pale hospitalini?”

“Yaani weee acha tu, hili sekeseka baba nahisi lina mtandao mkubwa sana. Kumbe makamu wa raisi bwana alitaka kumuua raisi Mtenzi”

“Wee”

“Haki ya Mungu vile na hapa bado ana endelea kumsaka ili amuue. Yaani hii ni siri kubwa sana ambayo endapo ita sikika kinywani mwa mtu basi ni lazime auwawe kikatili sana”

“Mmmm sasa una taka kuniambiwa, Magreth ndioa aliye msaidia?”

“Ndio baba”

“Duuu”

“Sasa hivi pale alipo mume wangu, akili yake haipo sawa kabisa. Nimemshauri tukodishe watu ambao wata muua makamu wa raisi, huku mzee akiendelea kufanyiwa maombi”

“Anafanyiwa maombi na nani?”

“Josephine sijui nani, kitu kama hicho”

“Kama ni Josephine ana weza kupona”

“Una mjua?”

“Ndio ni muumini wangu pale kanisani”

“Sasa baba tuna mpatia wapi mtu ambaye ana weza kudili na hili jambo na mbaya zaidi makamu wa raisi ameungana na yule mshenzi Evans na tulimkuta ikulu.”

“Ohooo!!”

“Ndio hivyo na walivyo kutana na mume wangu walizipiga kisawa sawa”

“Usiniambie”

“Ohoo yaani mtiti wake baba haukuwa mdogo kabisa. Hembu niambie ni nani ambaye tuna weza kumpatia hii kazi”

“Kuna Mmexcan mmoja naa itwa Frenando Machete. Ni professional killer, ni mmoja wa watu ninao wafahamu tuna weza kumpatia hiyo kazi”

“Ana weza hiyo kazi?”

“Sana kama kwenye asilimia basi nina mpa asilimia tisini na tisha pointi tisa”

“Sawa, wasiliana naye ili kama aikiwezekana aweze kuja nchini hapa kuikamilisha kazi hiyo”

“Poa ila kazi zake ana zifanya kwa garama kubwa sana”

“Wewe muite tu kwani pesa ni kitu gani baba. Kikubwa nina hitaji kumuaminisha mume wangu kwamba mimi ni mtu mwema, ikiwa haya yote yaliyo tokea una jua chanzo ni mimi”

“Chanzo ni wewe kivipi?”

“Una kumbuka wale askari walio lipuka na boti kipindi kile baharini?”

“Yaa”

“Sasa kuanzia pale raisi si alitoa agizo la Al-Shabab kushambuliwa?”

“Ndio, sasa hapa ndio napata picha. Ila hili jambo usimumbie mtu yoyote kwa maana uta uwawa”

“Weee ni wewe peke yako ndio nime kuambi hili swala baba, ila sinto fungua kinywa changu kumuambia mtu wa aina yoyote”

“Pia mume wangu usimueleze kitu chochote kuhusiana na ogarnaization yako?”

“Usijali baba”

“Ngoja nikaafute diary yangu kwa maana ndipo nilipo andika namba za watu wangu muhimu”

“Sawa”

Wakaingia ndani na Magreth akamfwata Jery sehemu alipo kaa huku nabii Sanga akielekea chumbuani kwake. Akamkuta mke wake akiwa amejilaza kitandani.

“Una jisikiaje?”

“Namshukuru Mungu nipo poa”

Nabii Sanga akafungua shelf yake iliyo jengewa ukutani. Akatoa diary yake ambayo ina namba za watu muhimu sana. Akaitafuta namba ya Frenando Machete na akaipata, akainakili kwenye simu yake na kuipiga. Simu ya Franando ikaanza kuita kisha ikapokelewa.

“Ni mimi”

Nabii Sanga alianza kuzungumza hivyo na Frenando aliweza kumfahamu.

“Ume salimikia nabii Sanga?”

“Ndio, nina mshukuru Mungu nime salimika. Upo wapi?”

“Nina jiandaa kuelekea Colombia. Kuna matembezi mafupi nina kwenda kuyafanya”

“Nina kuhitaji Tanzania?”

“Air port yenu ime salimika?”

“Ya Dar es Salama imefungwa kwa muda, ila wana tumia ya KIA”

“Ahaa hapo nime kuelewa. Una nihiyaji kwa lini?”

“Ikiwezekana hata kesho uwe ume fika nchini Tanzania”

“Basi sawa, naghairi kuelekea Colombia, nina kuja Tanzania. Bado una ishi pale pale au ume hama?”

“Nipo hapa hapa ulipo niacha”

“Sawa, siku njema”

“Nawe pia”

Nabii Sanga akakata simu na kuirudisha diary hiyo ndani ya shelf hiyo.

“Ni nani huyo mume wangu”

“Machete”

“Ana kuja kufanya nini Tanzania?”

“Mke wangu kuna jambo moja kubwa sana linalo endelea hapa nchini. Nina hitaji kumsaidia Jery katika hili”

“Jambo gani?”

“Una weza kuamini kwamba mtu aliye hitaji kumua raisi Mtenzi ni makamu wake wa raisi bwana Jr Madenge”

“Weee!!”

“Haki ya Mungu vile na hapa Julieth ndio ame toka kunieleza juu ya hilo. Sasa nina hitaji kumleta Machete adili na makamu wa riasi na hili la Al-Shaba, nina imani tuta dili nalo kwa upande mwengine wa shilingi”

“Ila hawa wapumbavu, kila nikiwafikiria vijana wangu nina ishiwa na nguvu. Haki ya Mungu nia hitaji hao Al-Shabab wakikamatwa, nimue kiongozi wao kwa kumkata kata kwa mapanga”

Mrs Sanga alizungumza kwa uchungu huku machozi yakimwagika usoni mwake. Taratibu nabii Sanga akaka pembeni ya mke wake na kumkumbatia kwa maana wote wapo kwenye kipindi cha majonzi kwani wame poteza watoto, ndugu, jamaa na wazazi katika mlipuko ulio tokea siku ya harusi ya binti yao kipenzi Julieth.

***

“Evans una paswa kufanya jambo sasa”

Jini Maimuna alizungumza huku akiwa amejawa na wasiwasi mkubwa sana.

“Jambo gani?”

“Ina kubidi umuue Jery, Magreth, Julieth na Josephine. Hao watu wakibaki hapa duniani kila jambo lina weza kuharibika na tukajikuta tuna poteza kila kitu kwa maana Josephine ana uwezo wa kunidhibiti mimi”

Jini Maimuna alizidi kuzungumza huku akiwa amejawa na huzuni kubwa sana.

“Sasa nita wauaje hao watu kwa maana sina uwezo wa kupambana sana”

“Tumia akili, kwani kuna wauaji wangapi wenye uwezo wa kufanya mauaji kwa watu na wakalipwa. Pesa ipo una taka nini cha ziada”

“Mmmm!!”

“Ndio fanya hivyo una siku sana na hatuto onana kwenye hizo siku saba hadi pale utakapo kamilisha hilo jambo kwa maana sasa hivi Josephine yupo kwenye maombi ya kuniangamiza na nikiangamizwa nina rudi gerezani”

“Gerezani wapi?”

“Kuzimu, na sinto kuwa na uwezo wa kuweza kutoka kabisa. Kwaheri”

Jini Maimuna akapotea ndani ya gari hilo la Evans na kumuacha akiwa katika wasiwasi mkubwa sana kwa maana huyo jini ndio tegemezi lake na fujo na jeuri aliyo nayo ni kutokana na jini Maimuna. Evans akasimamisha gari lake kwenye moja ya dula ambalo mtaa wake ume salimika kwa milipuko ya mabomu. Akanunua sofa moja na kuanza kunywa taratibu huku akitazama watu wanao katiza katiza kwenye mtaa huo.

“Hawa jamaa ni washenzi sana”

Muuza duka ambaye ana asili ya kichaga alianza kuzungumza na kumfanya Evans kutazama kama ni yeye ndio anye ongeleshwa au laa.

“Una zungumza na mimi?”

“Ndio kaka, hawa jamaa walio jilipua kwa kweli wame tuangamizia Watanzania wezetu wengi sana”

“Ndio hivyo ndugu yangu, kila unapo pita ni misiba mfululizo, watu wana lia kwa kupoteza ndugu zoa”

“Nina sikia kwamba ni hapa hapa Dar ndio wame shambuli?”

“Yaa kwa maana nime toka mkoa wa Morogoro, ila hawajashambulia”

“Daaa sijui itakuwaje kwa kweli”

“Hatuna la kufanya zaidi ya kumuomba Mungu atupe nguvu za kusonga mbele”

“Ni kweli kaka”

“Shukrani kwa soda”

Evans akairudisha chupa hiyo ya soda kisha akaingia kwenye gari lake na kuondoka. Akatafuta hoteli ambayo imesalimia, katikati ya jiji la Dar es Salaam na akafanikiwa kuipata. Akalipia chumba kimoja na kuingia ndani na kuanza kufikiria mpango wa kuwaua watu hao watono alio pewa kazi ya kuwaau na jini Maimuna.

***

“Jery na mke wake hawajarudi?”

Bwana Madenge Jr alimuuliza mmoja wawalinzi wake.

“Ndio muheshimiwa”

“Huyu mtoto amechananganyikiwa kweli?”

“Ana haki ya kuchanganyikiwa muheshimiwa kufikwa na mama yake na kupotea kwa baba yake ni pigo moja kubwa sana”

Mlinzi huyo alizungumza huku wakitazama bustani kubwa ya maua iliyopo eneo hilo la ikulu. Ujume mfupi wa meseji ukaingia kwenye simu ya bwana Madenge, akaitoa simu yake mfukoni na jambo la kumshangaza ujumbe huo ume toka kwa namba isoyo onekana(private number).

‘Zawadi ya kichwa ume ipata kuna zawadi yako nyingine ninayo’

Bwana Madenge Jr akajikuta akianza kutetemeka mwili mzima kwa wasiwasi kwa maana hajui ni nani aliye tuma ujumbe huo. Ikaingia ujumbe mwengine kwa njia ya whatsApp, ujumbe huo ni wa sauti akamtazama mlinzi huyo ambaye sio mtu anaye fahamu siri zake. Akasogea umbali kidogo na kuufungua ujumbe huo. Akaanza kusikiliza mahojiano ya kijana wake akuhojiwa na sauti ya ajabu kidogo ambayo hajawahi kuisikia kwenye maisha yake. Kijana wake ambaye kwa sasa ni marehemu alijikuta akitoa siri zote za mpango wa kumuua raisi Mtenzi.

‘Mungu wangu’

Bwana Madenge alizungumza huku mwili mzima ukimtetemeka kwa wasiwasi, hakujua mtu huyo ni nani. Ukaingia ujumbe mwengine wa maandishi.

‘Kabla sijauachia ujumbe huu kwenye vyombo vya habari nina hitaji kuonana na wewe. Nitakuambia siku na saa ya wapi mimi na wewe tuonane na endapo uta mjulisha mtu yoyote siri yako ita zidi kuvuja’

Bwana Madenge Jr akahisi kama moyo wake una kwenda kupasuka kwa maumivu makali, hakutarajia kama siri yake ime julikana kirahisi hivyo.

***

RPC Karata mara ya kumpa vitisho hivyo makamu wa raisi, akashuka kwenye gari lake, kabla hajaminya kitufe cha kengele mlangoni mwa nyumba ya Magreth. Magreth akafungua geti dogo na akatoka.

“Nilikuona kaka”

Magreth alizungumza huku akionyesha kamera zilizopo hapo getini kwake.

“Ahaa sawa sawa. Tuna weza kuzungumzia hata hapa nje”

“Sawa”

Wakaingia kwenye gari la RPC Karata.

“Leo huja tembea na mlinzi wako?”

“Nime mpa ruhusa ya kwenda kumzika shemeji yake kwani naye ame farika kwenye milipuko hii”

“Aisee mpe pole sana”

“Nashukuru. Ehee niambie Jery na mke wake walisemaje?”

Magreth akamuadiasia RPC Karata kila kitu alicho fanya na Jery pamoja na Julieth.

“Nina imani watakuwa na mpango juu ya kufanya jambo kwa makamu wa raisi?”

“Hata mimi nina hisi hivyo kaka”

“Sasa nime mpatia vitisho makamu wa raisi. Nina hitaji kuonana naye ila sija muambia muda wa yeye kukutana nami. Je una shauri nini?”

“Kama ni hivyo huo ndio wa kati wa sisi kumuua. Wewe panga ni wapi tuna kutana naye mimi nita ifanya hiyo kazi ya kumuua na siku hiyo nina kuhakikishia kwamba hato pona hata akija na askari mia moja ni lazima nimuue tu”

Magreth alizungumza kwa kujiamini na kumfanya RPC Karata kwani hata yeye akilini mwake ana waza kumuangamiza makamu wa raisi ambaye ana endelea kuiwinda roho ya raisi Mtenzi ambaye hadi sasa hivi hali yake ni mbaya na hajulikani kama ata pona au atakufa.



“Mungu atufanikishe katikka hilo nahiataji kumpatia vitisho hadi akakili yake itakapo kaa vizuri ndio tumuue”

“Sawa kaka”

“Basi acha nikaendelee na majukumu”

Magreth akashuka kwenye gari hilo na RPC Karata akaondoka eneo hilo. Magreth akarudi ndani huku akijaribu kutafakari mpango wa kumuondoa makamu wa raisi ili nchi ipate kuwa kwenye usalama mzuri.

***

“Nipo getini kwako muheshimwa”

Frendando Machete alizungumza kisha akakta simu yake na kuirudisha mfukoni mwake. Geti likafunguliwa na nabii Sanga akatoka huku akiwa amejawa na tabasamu pana sana usoni mwake.

“Karibu sana Tanzania Machete”

“Nashukuru sana”

“Kwa nini sasa hukunipigia simu nije kukupoea KIA?”

“Natambua ni hali gani ambayo una pitia. Hivyo nikaona sio vyema nikaja kukusumbua. Ila pi anime weza kufika mwenyewe”

Nabii Sanga na Frenando Machete wakakumbatiana na kuingia ndani.

“Shemeji habari za masiku?”

Franando Machete alizungumza hukuwakipeana mikono na mrs Sanga.

“Nashukuru shemeji. Habari za muda mrefu?”

“Nina mshukuru Mungu kwa kweli. Aiseee Julieth ndio ame kua mkubwa kiasi hichi?”

Mr Machete alizungumza huku akimtazama Julieth kwa tabasamu pana sana.

“Ndio na ameolewa”

“Kipindi kile nina ondoka kalikuwa bado kadogo sidhani kama una nikumbuka.”

“Nakukumbuka vizuri tu anko. Shikamoo”

“Marahaba. Huyu ndio mume wako?”

“Ndio ana itwa Frank. Frank huyu ni ak wangu ana itwa Machete”

“Nashukuru kukufahamu mjomba”

“Asante nawe pia”

Wakapata chaku cha mchana kwa pamoja kisha bwana Machete na nabii Sanga wakaondoka kuelekea katika hospitali ya Muhimbili.

“Ndugu yangu ni msoba mkubwa sana nilio upate. Nimepoteza ndygu zangu na mbaya zaidi nime poteza vijana wangu wawili wa kiume yule wa kwanza na wapili”

Nabii Sanga alizungumza kwa sauti ya upole huku machozi yakimlenga lenga usoni mwake.

“Pole sana ndugu yangu. Hayo ndio matatizo ya kimaisha”

“Ni kweli aisee, ila nina hasira snaa na hawa watu walio sababisha vifo vya wanangu na ndugu zangu”

“Utanipatia listi na nita dili na mmoja baada ya mwengine”

“Sawa ndugu yangu”

Wakafika hispitali ya Muhimbili na moja kwa moja wakaelekewa katika jengo la kuhifadhia maiti. Wakaanza kupitia maiti moja baada ya nyingine za familia ya nabii Sanga.

“Huu una onekana ulikuwa ni mpango wa muda mrefu”

“Ni kweli ndugu yangu kwa maana laiti kama wangekuwa wameshambulia sisi pale hotelini basi tunge jua wana nia ya kutuua sisi tu. Ila wameshambulia maeneo mengi ya jiji la Dar es Salaam”

“Duuu si AL-Shabab?”

“Ndio ni wao”

“Hawa kudili nao moja kw amoja ni jambo gumu sana isitishe ni kundi kubwa. Vipi wewe kundi lako lina fanya kazi gani sasa hivi?”

Mr Machele alizungumza wakitoka katika jengo hilo.

“Nime mrithisha mwanangu?”

“Yupi?”

“Julieth?”

“Ana iweza kazi au ume mrithisha kwa sababu ni mwanao wa mwisho?”

“Ana iweza kazi”

Mr Machete akamtaza kwa sekunde kadhaa nabii Sanga kisha akashusha pumzi nyingi.

“Nina mashaka na nafasi yake”

“Kwa nini?”

“Mtoto wa kike kama Julieth na aliye olewa ni ngumu sana kuongoza kundi kubwa la drugs delers kama hilo la kwako. Madhara yake ni makubwa sana”

Nabii Sanga akashusha pumzi taratibu huku akikumbuka kauli ya Julieth kwamba yote haya yaliyo tokea chanzo ni yeye.

“Ila tuyaache hayo. Ni nani ambaye ume niitia niweze kumuhamisha makazi”

Nabii Sanga akafungua mlango wa gari lake na wakaingia ndani.

“Yule kijana pale nyumbani ni mtoto wa raisi ambaye kwa sasa ame athiriwa katika shambulizi hilo la bomu.”

“Una taka kuniambia kwamba raisi wa Tanzania ame fariki?”

“Hapana ila ana pigania uhai wake, ila mke wake ndio aliye fariki”

“Aisee”

“Ila katika harakati za kuokoa maisha ya raisi. Makamu wake wa raisia ameonekana kuingiwa na tamaa ya madaraka na alihitaji kumuu kabisa raisi”

“Mungu wangu!!”

“Yaa hivyo kijana ame kusudia kuhakikisha kwamba ana muangamiza makamu wa raisi na kazi hiyo mtu wa pekee ambaye una weza kuifanya ni wewe”

“Sawa ina bidi nianze kupata data za ndani kabisa katika ikulu ili kama ni kumuondoa raisi iwe ni jambo raisi kwangu”

“Ina bidi tutafute kwa maana toka litokee hili shambulizi, kuna baadhi ya viongozi wame fariki huku wengine wakiwa wame kimbia kabisa mji. Hivyo kuweza kumpata mtu wa ndani kabisa ita kuwa ni jambo gumu sana”

“Basi usijali nipe siku ya leo nita kuwa nime pata full data”

“Sawa”

Wakarudi nyumbani ila mr Machete hakuingia ndani akaondoka nyumbani hapo kwa nabii Sanga na kuelekea katika eneo ambalo ana imani kwamba ana weza kupata kila kitu kinacho endelea ndani ya ikulu ambayo kwa sasa ipo chini ya makamu wa raisi bwana Madenge Jr.

“Baba vipi ume mueleza?”

“Ndio kwa sasa ana fanya uchunguzi w akufahamu ni kipi kinacho endelea ndani ya ikulu. Ila muambie Jery asionekane onekana eneo la nje kw amaana hatujui nani ni mbaya. Ume nielewa?”

“Ndio nime kuelewa baba”

“Jambo jengine la kukumbusha usifanye maamuzi yoyote ya kutumia watu wa ndani ya organization pasipi kuniomba ruhusa kuanzia hivi sasa. Ume nielewa?”

Nabii Sanga alizungumza kwa msisitizo huku akimtazama Julieth usoni mwake.

“Nime kuelewa baba ila nina weza kuuliza ni kwa nini?”

“Naamaini jibu unalo la kwa nini nime kuambia hivyo”

Nabii Sanga mara baada ya kuzungumza maneno hao akaingia ndani na kumuacha Julieth akiwa amejawa na mshangao mkubwa sana.

***

Makamu wa raisi bwana Madenge Jr, akazidi kuongeza ulinzi katika eneo zima la ikulu. Woga wa vitishoa alivyo vipata hakika vina mkosesha amani kwani asipo kuwa makini basi ana weza kufa.

‘Nani wa kunisaidia?’

Bwana Madenge aliwaza huku akizunguka zunguka ndani ya ofisi yake. Akilini mwake akamkumbuka Evans Shika amabye kwa sasa ana muona ndio mtabiri wake mzuri wa mambo yajayo au yalio fanyika kisiri. Akampigiaa simu Evans na kwa bahati nzuri simu hiyo ikapatikana.

“Shikamoo muheshimiwa”

“Marahaba, upo wapi?”

“Nipo hotelini”

“Una usafiri?”

“Ndio muheshimiwa”

“Njoo sasa hivi ikulu”

“Sawa muheshimiwa”

Makamu wa raisi akakata simu na kuendelea kuchanganua ni kitu watu gani ambao wame weza kumuua kijana wake. Akayasikiliza mazungumzo aliyo tumiwa kwenye simu yake kwa mara nyingine jinsi kijana wake akikiri siri ambayo hakupenda iweze kutoka kwa mtu wa aina yoyote.

‘Huyu mshenzi ni lazima nimkamate’

Alizungumza kwa hasira sana. Baada ya dakika arobaini, Evans akafika ofisini hapo huku akiwa ameongozana na walinzi wawili.

“Muna weza kutuacha”

Bwana Madenge aliwaambia walinzi hao na wakatoka ofisini hapo.

“Nina tatizo”

“Tatizo gani muheshimiwa?”

“Kuna mtu ana nitishia maisha yangu na anataka kunia”

“Mungu wangu ni nani huyo?”

“Nime kuita hapa ili weze kuniambia huyo mtu ni nani na ana kaa wapi ili kama ni kumshuhulikia basi niweze kumshulikia leo hii hii?”

Mapigo ya moyo ya Evans yakaanza kumuenda kasi hadi akatamani ardhi ipasuke na immeze, kwani hawezi kufanya kitu chochote pasipo uwezo wa msaada kutoka kwa jini Maimuna.

“Huyo mtu aliye taka kukuua amekupigia simu au?”

Evans alizungumza kwa kujikaza huku mapigo yake ya moyo yakimuenda kasi sana.

“Hajanipigia simu, ila jambo la kwanza walimchinja mlinzi wangu na wakaniletea kichwa hapa ikulu”

“Hapa hapa Ikulu?””

“Ndio, jambo la pili wakanitumia audio ya vitisho kwamba nita fwata mimi. Hembu fanya jambo juu ya hili”

Evans kwa haraka akakumbuka ni watu gani ambao jini Maimuna alimuambia kwamba wana paswa kufa kabla ya wiki hii.

‘Hii ndio nafasi ya kuwagonganisha’

Evans alifumba macho yake taratibu akiigiza kana kwamba ana omba jambo fualani. Akayafumbua macho yake na kumtazama makamu wa raisi bwana Madenge Jr.

“Muheshimiwa kuna watu wanne ambao ndio wana iwinda roho yako na watu hao ume weza kuwasogeza karibu yako”

Evans alijifanya kuzungumza kwa sauti nzito kana kwamba ana jini ndani yake.

“K…i…in….a nani hao?”

“Wa kwanza ni Jery Mtenzi, wa pili ni Julieth Sanga. Watatu ni Josephine na wanne ni Magreth”

Makamu wa raisi macho yakamtoka kwa mshangao mkubwa sana kwani hao wote walio tajwa, wawili ana waoana ni watumishi wa Mungu walio shiba sana neno la Mungu na hao wawili ni kapuku tu ambao hawaa uwezo wa kumfanya jambo lolote mbele yake.

“Wewe ume changanyikiwa au?”

Makamu wa raisi aliuliza kwa ukali huku akimtazama Evans kwa macho makali sana.

“Hicho ndio nilicho onyeshwa mkuu amini usiamini ila hao ndio watu wanao iwinda roho yako”

Makamu wa raisi akashusha pumzi huku mapigo yake ya moyo yakianza kumuenda kasi.

“Kwa nini wahiyaji kuniaua?”

“Ukiwakamata nina imani wana weza kukueleza ni kwa nini wana hitaji kukuua”

Mlango ukagongwa na sekretari akaingia ndani hapo.

“Muheshimiwa wageni wamesha fika”

“Wakaribishe ndani. Kijana nina kuomba unisubirie bado sija maliza na wewe”

“Sawa”

Evans akatoka ndani hapo na akapishana mlangoni na wanajeshi wawili wa Kimarekani ambao wame valia kombati za jeshi la nchi hiyo.

“Habari muheshimiwa raisi”

“Salama karibuni sana Tanzania”

“Tuna shukuru sana muheshimiwa. Pole sana kwa matatizo”

“Tunashukuru”

Evans akamfwata sekretari wa makamu wa raisi.

“Samahani dada”

“Bila samahani?”

“Hawa wanajeshi wametoka wapi?”

“Marekani?”

“Aha…una jua kwamba wame kuja kufanya nini?”

“Samahani kaka hizo ni ishu za kiserikali hivyo sipaswi kumuambia mtu yoyote”

“Ahaa….una jua mimi na muheshimiwa ni watu ambao tuna saidiana sana kwenye mambo mengi hivyo sio mbaya nikafahamu”

“Kaka samahani siwezi kuzungumza chochote.”

“Habari yako dada. Nina hitaji kumuona muheshimiwa raisi”

Sauti hiyo ikamfanya Evans kugeuka nyuma na kukutana na sura ya bwana Frenando Machete aliye valia ndevu za bandia huku kifuani mwake akiwa amening’iniza kitambulisho kinacho muonyesha kwamba yeye ni mfanyakazi wa shirika la umoja wa mataifa linalo fanya kazi ulimwenguni pote.



“Ahaa samahani una miahadi naye?”

“Hapana ila ni muhimu”

“Naomba kitambulisho chako”

Mr Machete akavua kitambulisho hicho na kumkabidhi sekretari huyo. Sekretari akaingiza namba ya kitambulisho hicho na baada ya muda sekunde kadhaa taarifa za mr Machete zikatokea kwenye computer yake. Taarifa zina onyesha kwamba yeye ni mkurugenzi msaidizi wa shirika hilo la UN kwa upande wa Afrika Mashariki.

“Makamu wa raisi kwa sasa ana wageni ila ninge omba uweze kumsubiria kama huto jali”

“Sawa sawa”

“Karibu ukae pale. Una hitaji nikupatie kinywaji gani?”

“Kahawa tafadhali”

“Sawa. Kaka nawe nisubirie pale nikuletee kinywaji gani?”

“Maji ya kunywa?”

“Baridi au moto?”

“Nahitaji ya baridi”

Sekretari huyo akaondoka eneo hilo na kuwaacha Evans na bwana Machete ambaye masaa mawili yaliyo pita aliweza kukutana na mdukuzi(hakers) ambaye mara nyingi huwa ana fanya kazi naye za kufoji vyeti vya mashirika mbalimbali ya usalama na mashirika makubwa. Hata hicho kitambulisho alicho pewa ni feki japo sio rahisi kwa mtu kuweza kugundua na taarifa zake ni ngumu sana kwa mtu kuelewa kwamba ni feki. Sekretari akawaletea kila mmoja kinywaji chake.

“Shukrani”

Bwana Machete alizungumza huku akianza kunya kahawa hiyo. Baada ya dakika ishirini na tano wanajeshi hao walio fanya mazungumzo na makamu wa raisi wakatoka huku wakiwa wameongozana na maakamu wa raisi. Wakaagana mbele ya Evans na bwana Machete.

“Kijana njoo”

Evans akasimama na kumfwata bwana Madenge ofisini kwake.

“Ehee una taka kuniambia kwamba hao ulio wataja ndio wana hitaji kunia mimi?”

“Ndio muheshimiwa?”

“Una weza kuniambia sababu zao wao kutaka kunia?”

“Sija jua, ila muheshimiwa sio kila anaye hitaji kumuua mtu ana kuwa sababu. Wewe mwenyewe una weza kuhushudia jinsi wana Dar es Salaam wengi walivyo kufa, je walikuwa na sababu ya wao kuuwawa?”

“Hapana”

“Basi tambua hilo”

“Wewe una nishauri nini?”

Sekretari akaingia ofisini hapo.

“Sahamani muheshimiwa kama nita kuwa nime kuvunjia mazungumzo yako”

“Bila samahani”

“Aliyopo hapo nje kwenye kiti ana itwa Fredy Martin ana ni director msaidizi kutoka UN ana hitaji kuzungumza nawe ni jambo la muhimu sana”

“Ohoo basi muambie aingie. Wewe Evans nenda nita jua nini cha kufanya”

“Nina shukuru sana muheshimiwa”

“Haya”

Evans akatoka ndani hapo huku akiwa na furaha sana moyoni mwake akiamini kwamba tayari amesha maliza kazi ya kuwagonganisha maadui zake na makamu wa raisi ambaye ana onekana kuamini kila jambo analo mueleza. Bwana Machete akaingia ndani hapo na wakasalimiana na makamu wa raisi.

“Karibu sana bwana Fredy”

“Nashukuru sana muheshimiwa makamu wa raisi. Poleni sana kwa matatizo yaliyo tokea?”

“Tunashukuru sana. Tuna endelea kulijenga jiji letu upya”

“Ni kweli”

“Ni nini kime kuleta ofisini kwangu bwana Fredy Martin”

Bwana Machete akamtazama makamu wa raisi bwana Madenge kwa muda kisha akatabasamu kwa maana ana uwezo wa kufanya jambo lolote hususani la kumuua akiwa hapo hapo ndani ya ikulu. Ila ulinzi alio kutana nao nje ya ikulu hakika una weza kumuweka katika mazingira magumu sana ya kushindwa kutoka ikulu hapo pamoja na nje ya nchi ya Tanzania.

“Nime kuja kuzungumzia juu ya msaada ambao tuna hitaji kuutoa kwenye serikali yako kwa haya majanga yaliyo tokea hususani kwa wananchi walio poteza makazi yao. Viongo na wengine kufariki kabisa. Hivyo kama uta kubaliana na ofisi yangu basi tuna weza kukusaidia katika hilo?”

“Nipo tayari na milango ya nchi yangu ipo wazi kabisa kuwakaribisha kuhakikisha kwamba tuna shirikiana kwa pamoja kuisimamisha nchi kwa wakati mwengine kwa maana jiji hili ndio kitovu kikuu cha biashara hapa Tanzania”

“Basi hakuna shaka muheshimiwa. Nita rudisha majibu ofisini kwangu kisha tuta kuja kujadili ni maeneo gani ambayo kama serikali yako ita hitaji tuuweze kuchukua nafasi ya kukusaidia”

“Sawa nipende kuwashukuru sana kwa uwepo wenu”

“Sawa muheshimiwa”

Mr Machete kabla ya kunyanyuka kwenye kiti hicho akaingiza mkono wake mukoni na kufasua pati yenye sumu inayo weza kumuua mtu ndani ya dakika ishirini na tano. Sumu hiyo iliyo katika kmfumo wa mafuta malaini na endapo mtu akiguswa na mafuta hayo basi ana uwezo mkubwa sana wa kufa ndani ya muda mchache. Mr Machet alipo hakikisha kwamba amajipaka vizuri kiganja chake mafuta hayo. Akautoa kisha akasimama, huku tabasamu likiwa ni pana sana uosni mwake.

“Muheshimiwa mimi acha niende na shukrani sana kwa ukarimu wako”

Makamu wa raisi pasipo kufahamu chochote akapena mkono na bwana Machete. Kisha wakatoka nje ya ofisi hiyo na wakaagana tena mbele ya sekretari pamoja na wana usalama wawili waliopo eneo hilo.

“Liliy”

“Ndio muheshimiwa”

“Nahitaji kupumzika sasa hivi sinto hitaji mgeni yoyote hata awe wa muhimu”

“Sawa muheshimiwa”

Makamu wa raisi akarudi ndani ya ofisi yake na kujilaza kwenye sofa huku akijaribu kutafakari ni kitu gania mbacho ana weza kukifana ili kuhakikisha kwamba ana fwata ushari alio pewa na Evans. Mr Machete mara baada ya kuingia kwenye gari lake lenye namba za UN pamoja na nembo ya shirika hilo. Akatoa sindano pamoja na kichupa kidogo, kwa haraka akavuta dawa ambayo ina uwezo wa kuua makali ya sumu hiyo ndani ya dakika kadhaa. Akajichoma mkono wake wa kushoto dawa hiyo na taratibu akaanza kujihisi unafuu kwa maana tayari mwili wake ulisha anza kuvunjwa na jasho jingi ikiwa ndio dalili ya kwanza kabisa yaletwayo na sumu hiyo. Akawasha gari lake na kuondoka eneo hilo la ikulu pasipo kutiliwa mashaka ya aina yoyote.

“Sanga”

“Ndio”

“Nina ondoka kazi yako tayari”

Bwana Machete alizungumza kwa kutumia simu yake ya mkononi.

“Kweli?”

“Ndio baada ya muda uta pata majibu”

“Ila ndugu yangu si ungekuja tuonane kidogo?”

“Hapana naamini una jua uhatari wa hii kazi hivyo sinto weza kukaa nchini kwa sasa. Tuwasiliana nikifika kiwanja cha ndege”

“Sawa bwana nikuingizie pesa kwenye akaunti ipi?”

“Ile unayo niingizia”

“Sawa nafanya hivyo muda si mredu”

“Nashukuru”

Bwana Machete akakata simu na kuendeleea kuliendesha gari hilo kwa mwendo wa kasi kuhakikisha ana toka jiji la Dar es Salaam kabala ya mambo hayajawa mabaya kwa upande wake.

***

Kila dakika zinavyo zidi kwenda bwana Madenga akaanza kujihisi hali ya utofauti ambayo hakika hakuwahi kuipata toka kuzaliwa kwake. Jasho jingi likazidi kumtiririka mwilini mwake japo kuwa ndani ya ofisi yake kuna IC yenye ubaridi mkali.

“Lily”

Bwana Madenge aliita kwa tabu sana huku akihisi kizunguzungu kikali sana.

“Lily….”

“Huyo anaye ita ni bosi?”

Lily aliwauliza walinzi hao ambao hawakuhitaji kujishauri mara mbili wakafungua mlango huo na kumkuta bwana Madenge akiwa anajaribu kunyanyuka ila ana shindwa.

“Muheshimiwa una nini?”

Lily aliuliza huku akiwa amejawa na wasiwasi mkubwa.

“Hata sijui najisikia vibaya sana”

Lily na walinzi hao wakaanza kushangazwa na jinsi makamu wa raisi anavyo mwagikwa na machozi yaliyo changayikana na damu.

“Mungu wangu”

Lily aliweweseka kwa haraka, daktari wa ikulu akafika eneo hilo na kuanza kumpima makamu wa raisi ambaye hali yake ina zidi kuwa mbaya.

“Ina bidi tumuwahishe Muhimbili haraka iwezekanavyo”

Daktari alizungumza na wakapiga simu kwenye kitengo kinacho husika na usafiri wa anga ambao ni helicopter ya raisi. Kitanda cha magurumu kikaletwa ofisini hapo, wakamlaza bwana Madenge na wakaanza kumsukuma huku daktari akijaribu kutoa huduma ya kwanza.

“Moja mbili tatu”

Walinzi hao walihesabu na kukikanyanyua kitanda hicho na kukiingiza ndani ya helicopter hiyo kubwa. Yenye uwezo wa kubeba watu kumi na tano. Safari ya kuelekea hospitali ya Muhimbili ikaendelea huku hali ya bwana Madenge Jr ikizid kuwa mbaya kwani sasa damu zilianza kumtoka hadi masikioni. Wakapokelewa hospitali ya Muhimbili na moja kwa moja wakampeleka bwana Madenge katika chumba maalumu cha matibabu. Madaktari waakaanza kumuwekea mashinde za kumsaidia kuhema, ila kabla hata hawajaanza matibabu bwana Madenge Jr akaaga dunia.

Madaktari sita waliomo ndani ya chumba hicho wakatazamana huku kila mmoja akiwa na wasiwasi mkubwa. Kitendo cha viongozi wawili wakubwa wa taifa kufariki ndani ya wiki moja ni jambo baya sana kwa taifa.

“Toka nianze maisha yangu ya udaktari huu ni mwaka wa thelathini ila sijawahi kuona ugonjwa kama huu”

Daktari mkuuwa kikosi hicho alizungumza huku akiwatazama wezake

“Au ni Ebola?”

“Hapana sio Ebola, hembu chukueni vipimo vya damu yake ili tuweze kufahamu ni kitu gani kime muua. Ila taarifa hii ya kifo musiizungumze kwa mtu yoyote hadi pale tutakapo pata mtu sahihi wa kumueleza hili”

“Sawa dokta”

Dokta Emanuel ambaye ndio mkuu wa kikosi hicho akatoka ndani hapo na kukuatana na Lilian pamoja na walinzi walio mleta makamu wa raisi eneo hilo.

“Daktari hali ya muheshimiwa ina endeleaje?”

Lilian aliuliza huku akiwa amajawa na mashaka mengi sana.

“Ahaa kwa sasa tuna endelea kumshulikia tuta wapa ripoti yake muda sio mrefu”

“Sawa dokta”

“Ahha muna weza kuwasiliana na waziri mkuu?”

“Ndio”

“Basi wasiliana naye ili aweze kufika hapa hospitalini”

“Sawa doctor”

Lilian akawasilina na waziri mkuu na akaahidi atafika hospitalini hapo baada ya nusu saa.

***

Josephine akazidi kusali hukua kiwa amepiga magoti pembezoni mwa kitanda alicho lazwa raisi Mtenzi. Gafla hali ya chumba ikaanza kubadilika na joto kali likaanza kutawala. Josephine hakutishwa na hali hiyo zaidi alicho zidi kukifanya ni kuhakikisha kwamba ana endelea kusali kwa juhudi zake zote. Gafla akastuka akishikwa mkono wake na kujikuta akifumbau mcho yake huku akiwa amejawa na woga mwingi sana.

Macho yake yakagongana na macho ya raisi Mtenzi.

“Hei”

Raisi Mtenzi aliita kwa sauti ndogo na iliyo jaa unyonge mwingi sana. Tabasamu pana likamtawala Josephine usni mwake, akatamani kupiga yowe ala furaha ila akakumbuka kwamba pasipo kumshukuru Mungu kwa muujiza huo basi mambo yana weza kuharibika.

“Asante Mungu baba, asante Jehova, nime ona ukuu wako, nimeona nguvu zako. Hakika jina lako lihimidiwe”

Josephine alizungumza huku machozi yakimwagika sana usoni mwake.

“Nipo wapi binti?”

“Upo nyumbani kwa rafiki yangu. Mimi nina itwa Josephine ni mtumishi wa Mungu”

Raisi Mtenzi akaanza kuangaza angaza ndani ya chumba hicho. Akajitazama mwilini mwake na kujikuta akiwa amefunikwa shuka huku akiwa amevalishwa mavazi ya hospitalini.

“Karibu tena duniani muheshimiwa”

“Nashukuru. Ume sema una itwa nani?”

“Josphine”

“Nime fikaje fikaje hapa”

“Muheshimiw ani historia ndefu sana. Ila sifa zote tumrudishie Mungu kwa maana yeye ndio aliye tupa nafasi nyingine ya kukurudisha duniani”

“Kwani nilikuwa nime kufa?”

“Hapana muheshimiwa ila ulikuwa ume karibia kufa”

Raisi Mtenzi akajikuta machozi yakimwagika, akazidi kukishika kiganja cha mkono cha Josephine kwa msisitizo.

“Nina shukuru sana binti”

“Usinishukuru mimi muheshimiwa. Sifa zote ni kwa Mungu”

“Ni kweli naomba uniitie mke wangu. Nahitaji kuzungumza naye”

Kauli hiyo ya raisi Mtenzi ikamfanya Josephine kupatwa na kigugumizi kwa maana ana tambua wazi, mrs Mtenzi kwa sasa ni marehemu na endapo ata mueleza juu ya ukweli huo basi ina weza kumletea matatizo makubwa raisi Mtenzi.



“Ahaa muheshimiwa kwa sasa pumzika kwanza. Acha nikuletee chakula”

Josephine alizungumza kwa furaha kisha akanyanyuka na kutoka ndani hapo.

“Vipi?”

Magreth aliuliza kwa msutuko mara baada ya kumuona Josephine akiwa sebleni hapo.

“Amepona. Muheshimiwa amepona”

Juma, Magreth na dokta Masawe wakajawa na furaha kubwa huku kila mmoja akiwa na shahuku ya kutaka kumuona dokta Masawe akawa wa kwanza kuingia ndani hapo.

“Muheshimiwa raisi”

Dokta Masawe alizungumza huku akiwa amejawa na tabasamu pana sana usoni mwake.

“Masawe”

“Ndio muheshimiwa. Unajisikiaje?”

Magreth na Juma nao wakaingia ndani happ na kumfanya raisi Mtenzi kushangaa.

“Nyinyi ni kina nani?”

Raisi Mtenzi alizungumza na kumfanya dokta Masawe kumtazama Magreth.

“Muheshimiwa mimi nina itwa Magreth, Ni mfanyabishara wa daraja la kawaida. Hapa ni nyumbani kwangu. Huyu ni Juma ni mfanyakazi wangu na huyu ni dokta Masawe”

“Masawe mimi nina mfahamu. Familia yangu ipo wapi?”

“Nampigia simu Jery aweze kufika hapa kwa maana nina namba yake”

“Hapa ni wapi?”

“Kigamboni muheshimiwa?”

“Kwa nini sipo ikulu?”

“Ni stori ndefu muheshimiwa ila tuna omba muheshimiw aniwasiliane na Jery kisha tuta zungumza kwa kina”

Magreth alizungumza, akaitoa simu yake mfukoni, kabla hata hajampigia Jery akasikia kengele ya getini kwake ikiita. Akaingia upande wa cctv kamera ambazo ana weza kuzitazama popote alipo kupitia simu yake ya mkononi. Akamuona Jery akiwa amesimama getini kwake.

“Jery amesha fika hapa”

Josephine alizungumza na akatoka ndani hapo. Akafungua geti na kusalimiana na Jery.

“Ume kuja peke yako?”

“Ndio”

Jery akaingiza gari hilo alilo kuja nalo.

“Vipi hali ya baba?”

“Amezinduka?”

“Kweli?”

“Ndio”

Jery kwa haraka haraka akaongoza njia na kuingia ndani ya chumba alichopo baba yake. Hakuamini macho yake kumuona baba yake akiwa amekaa kitako kitandani hapo. Akamfwata na kumkumbatia, huku akimwagikwa na machozi.

“Hei hei, Jery vipi mbona un alia”

Magreth akatoa ishara kwa Juma na dokta Masawe na wakatoka ndani hapo ili kuwapa nafasi Jery na baba yake kuzungumza.

“Baba hali yako haikuwa nzuri kabisa”

“Usijali mwanangu. Mungu amenisaidia nime weza kupona. Vipi hali ya mama yako?”

Jery akamtazama baba yake kwa sekunde kadhaa kisha machozi yakazidi kumbubujika. Ishara hiyo ikamdhihirishia raisi Mtenzi kwamba hakuna usalama kwa mke wake.

“Niambie ni nini kime mkuta mama yako?”

“Mama…..aa…..amamaa hayupo naye tena duniani”

Raisi Mtenzi akajawa na mshangao kama wa dakika tano, hakupepesa kabisa macho yake. Kity alicho kikumbuka siku ya harusi, alimuaga mke wake na kumuacha akiwa na wageni kisha yeye akaelekea gorofa ya juu walipo Jery na mke wake.

“Babab”

“Mmmm”

Raisi Mtenzi alistuka kidogo huku akimtazama Jery usoni mwake.

“Ni lazima baba ulipe katika hili”

“Lipi?”

“Kufa kwa mama”

Raisi Mtenzi hakujibu kitu chochote zaidi ya kuendelea kumuwaza mke wake huku machozi yakiendelea kumwagika kwa wingi usoni mwake.

***

Waziri mkuu akafika katika hospitali ya Muhimbili moja kwa moja akelekea katika ofisi ya dokta Emmanuel.

“Heshima yako mkuu”

“Nashukuru “

“Hembu niambie kuhusiana na hali ya makamu wa raisi bwana Madenge”

Dokta Emmanuel taratibu akashusha pumzi huku akimtazama waziri mkuu usoni mwake.

“Makamu wa raisi amefariki duninia?”

“NINI!!?”

“Ndio amefariki dunia”

“Kivipi ikiwa leo asubuhi alikuwa ofisini kwake na ana fanya kazi zake akiwa na afya nzuri”

Waziri Mkuu aliuliza kwa msisitizo mkubwa sana.

“Sijajua muheshimiwa ila tuna ufanyia vipimo mwili wake kisha baada ya hapo tuta kuwa na majibu kamili”

Waziri Mkuu akahisi kuchanganyikiwa, matatizo yame kuwa yakiwaandama viongozi wake wa ngazi za juu”

Mlango uka gongwa na dokta Emmanuel akamruhusu mtu huyo kuingia ndani. Akaingia daktari msaidizi.

“Muheshimiwa ripoti ya majibu haya hapa”

Dokta Emmanuel akachukua faili hilo haraka haraka na kulifungu. Akaanza kusoma maelezo hayo na kujikuta macho yakimtoka.

“Nini?”

“Ina onyesha kwamba makamu wa raisi aligusa sumu kali sana ambayo ilimshambulia kwa kasi ya ajabu sana na kuepekea umauti wake.”

“Hiyo sumu aliisusia wapi?”

“Hata mimi sifahamu muheshimiwa ila inaonyesha alishika sumu ambayo kwa kweli ndio mara yangu ya kwanza nime ishuhudia katia uuwaji ule”

“Ehhee Mungu mbona yanatokea sasa hivi”

“Ni pigo jengine kwa taifa”

“Hembu kanionyesheni mwili wake”

“Sawa muheshimiwa”

Wakatoka ofisini hapo na kuelekea katika chumba cha matibabu kwa maana bado mwili wa makamu wa raisi haujatolewa ndani hapo. Dokta Emmaunuel akalifunua shuka hilo eneo la sura ya makamu wa raisi. Waziri mkuu akajikuta akifumba macho kwani mwili wa makamu waraisi ume anza kuharibika.

“Kwa nini mwili wake ume anza kuharibika haraka kiasi hicho?”

“Hii sumu muheshimiwa kwa hapa Tanzania sijawahi kuina wala kuisikia na wala sifahamamu ina itwaje”

“Hamuna sindano ambayo ina weza kumsaidia kuto kuharibika kwa mwili wake?””

“Hapana muheshimiwa”

“Basi acha nilitangazie taifa na pia mazishi yake yaandaliwe haraka iwezekanavyo. Upelekeni mwili wake mochwari”

“Sawa muheshimiwa”

Waziri mkuu akatoka ndani hapo, akamtazama sektretari wa makamu wa raisi.

“Binti”

“Ndio muheshimiwa”

“Rudi ikulu uka niandalie mkutano na waandishi wa habri”

“Sawa muheshimiwa. Ila vipi hali ya makamu wa raisi?”

“Tuta waambia”

“Sawa”

Lily akaondoka hospitalini nabaadhi ya walinzi kwa kutumia helicopter ya raisi. Huku njiani akiwa na kazi ya kuwataarifu waandishi wa habari waweze kufika ikullu ndani ya muda huo.

“Kuna habari mbaya”

Waziri mkuu alimuambia mlinzi wake.

“Habari gani mkuu?”

“Makamu wa raisi ame fariki”

“Mungu wangu?”

“Ndio,amekufa kwa kushika sumu hivyo hatujui huiyo sumu ameweza kuishikia wapi.”

“Sasa uta fanyaje muheshimiwa?”

“Hata sifahamu”

“Muheshimiwa wewe sasa hivi kutokana na katiba ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania, wewe ndio raisi wa nchi”

Makamu wa raisi akashusha pumzi huku akimtazama kijana wake huyo.

“Illa kumbuka kwamba oparesheni ya kumtafuta raisi bado haijakwisha”

“Ni kweli, ila nchi haiwezi kwenda bila kiongozi. Tambua wewe ndio kiongozi wa ngazi za juu uliye bakia”

“Sawa acha tuangalie”

Waziri mkuu akaondoka hospitalini hapo akiwa na msafara wake na kuelekea ikulu.

“Nahitaji kuzungumza na mtoto wa makamu wa raisi”

“Sawa muheshimiwa. Acha nimpigie”

Msaidizi wake akampigia simu kijana huyo mwenye umri wa miaka ishirini na tano kisha akamkabidhi simu waziri mkuu.

“Ibra una zungumza na waziri mkuu hapa”

“Shikamoo muheshimiwa”

“Marahaba upo wapi?”

“Ahaa nipo Mbezi Beach nyumbani huku”

“Una weza kuja Ikulu muda huu”

“Ndio muheshimiwa”

“Basi njoo nina kusubiria”

“Hakuna shaka”

Waziri mkuu akakata simu na kumrudishia mlinzi wake. Wakfika ikulu na kukuta waandishi wa habari tayari wamesha kusanyika katika chumba cha habari. Waziri mkuu akamsubiria Ibra kufika hapo ikulu.

“Nashukuru kwa kuja”

“Nashukuru, najiribu kupiga namba ya mzee ila nina ona ime zimwa vipi yupo bize?”

“Hapana, kuna jambo nina hitaji kuzungumza nawe”

Waziri mkuu alizungumza kwa sautu ya upole.

“Nakusikiliza muheshimiwa”

“Baba yak oleo aliweza kushika sumu kali sana ambayo ilimpelekea kufariki duniani”

Ibra macho yakamtoka kisha akajikuta akitabasamu.

“Haupo serious muheshimiwa. Ashike sumu alafu afe pasipo kuila”

“Ni jambo la ukweli. Nimeona nikueleze wewe kabla sija kwenda kuzungumza na waandishi wa habari juu ya kifo cha mzee wako”

Ibra machozi yakaanza kumlenga lenga kwani leo asubuhi alizungumza na baba yake na alimuhakikishia kwamba sherehe yake ya kuzaliwa ambayo ni kesho ata ifanya hapo ikulu.

***

Bwana Machete akafika eneo la Chalinze alipo kijana Max ambaye asilini yake ni Mrusi.

“Max nina shukuru sana kwa kunisaidia”

Mr Machete alizungumza mara baada ya kushuka kwenye gari hilo lenye nembo ya UN.

“Wewe ni ndugu yangu na nipo kwa ajili yako. Ila mpango wako ume kwenda kama vile ulivyo hitaji?”

“Ndio na nina imani kwa sasa ata kuwa amesha kuwa mwenyeji Mbinguni”

“Safi sana nina imani kwamba ume ua kiprofessional?”

“Yaa sijawahi kukosea kazi yangu. Sasa nisaidie kufika CIA, si una fahamu kwamba siwezi kutumia gari hili”

Mr Machete alizungumza huku akibadua ndevu zake za bandia.

“Usijali acha nijiandea ili nikupeleke”

“Sawa”

Max akajiandaa haraka haraka, akachukua funguo ya gari yake aina ya Ford Ranger na kuondoka eneo hilo kwa mwendo wa kasi, wakiwa njiani hawakushangazwa kwa taarifa ya kifo cha makamu wa raisi kinacho tangazwa na waziri mkuu.

“Kazi nzuri sana kaka”

“Nashukuru”

Simu ya mr Machete ikaanza kuita, akaitazama na kukuta ni namba ya nabii Sanga.

“Upo very smart”

“Nashukuru bosi”

“Muamala wako tayari nina subiri uwe approved”

“Nashukuru sana boss”

“Safari nje”

“Nawe pia”

Mr Machete akakta simu na kumtazama Max anaye endesha gari hilo.

“Nita kuingizia asilimia ishirini ya kiasi nilicho pata”

“Shukrani kaka”

***

“Ni nini kime tokea?”

Magreth aliuliza huku wote wanne wakishangaa habari juu ya kifo cha makamu wa raisi, kwani ni mtu ambaye ni adui yao na Magreth alipanga kumuua ila mpango wake ume weza kuwahiwa na mtu asiye mfahamu hadi sasa.



“Hata mimi sifahamu nini kime tokea”

Juma alijibu kwa sauti ya upole huku naye akiendelea kuitazama taarifa hiyo inayo tolewa na waziri mkuu. Magreth akatoa simu yake mfukoni na akatoka ndani hapo. Akaitazama namba ya RPC Karata kisha akampigia.

“Kaka habari”

“Salama vipi hili lililo tokea wewe ndio ume husika?”

“Hapana hata mimi nilitaka kuluuliza kama wewe ndio ume lifanya?”

“Ila ngoja kwanza Mage nimekumbuka jambo”

“Jambo gani kaka?”

“Uliniambia kwamba Jery na Julieth kwamba walikuja hapo kwako?”

“Ndio na Jery yupo hapa kwangu sasa hivi na habari nzuri ni kwamba raisi amezinduka”

“Kweli?”

“Ndio”

“Basi nina kuja sasa hivi”

“Sawa”

Magreth akakata simu huku akishusha pumzi nyingi. Magreth kwa haraka akarudi ndani na moja kwa moja akaelekea katika chumba alipo Jery na baba yake.

“Samahani Jery tuna weza kuzungumza mara moja?”

Magreth alizungumza huku akimtazama Jery usoni mwake. Taratibu Jery akanyanyuka na wakaelekea sebleni.”

“Makamu wa raisi amefariki leo, je unatambua juu ya kifo chake?”

Jery macho yakamtoka, akamtazama Magreth kisha akamsikiliza waziri mkuu anaye endelea kuhutubia taifa juu ya kifo cha makamu wa raisi.

“Kuna nini kinacho endelea?”

Kila mtu akamgeukia raisi Mtenzi alite fika hapo sebeni pasipo mtu yoyote kumuona.

“Ahaa baba kuna….kuna taarifa kidogo una weza kurudi ndani mara moja”

“Muheshimiwa chakula kipo tayari”

Josephine alizungumza mara baada na yeye kufika sebleni hapo. Raisi Mtenzi akaendelea kuisikiliza taarifa hiyo huku machungu yakiendelea kumjaa moyoni mwake kwani rafiki yake na aliye muamini sana bwana Madenge ame fariki dunia. Magreth akatoka sebleni hapo mara baada ya kusikia kengele ya getini kugongwa. Akafungua geti na RPC Karata akaingia huku akiwa ameongozana na vijana sita wa kitengo cha kutuliza ghasia, FFU.

“Imarisheni ulinzi”

“Sawa mkuu”

Wakaingia sebleni, RPC Karata akasimama kwa sekunde kadhaa huku akiwa amejawa na tabasamu.

“Muheshimiwa”

Taratibu raisi Mtenzi akageuka na kumtazama RPC Karata.

“Karata”

“Ndio muheshimiwa”

“Una fahamu ni nani aliye husika na kifo cha makamu wa raisi?”

“Hapana muheshimiwa kifo chake kime tokea galfa tu na ina sadikika alishika sumu”

“Sumu ya aina gani?”

“Hata mimi sifahamu muheshimiwa”

“Ahaa baba makamu wa raisi sio mtu wa kumuamini kabisa”

“Kwa nini?”

“Alihitaji kukuua ndio maana hivi sasa upo hapa”

Jery alizungumza kwa kujiamini sana.

“Hapana Madenge hawezi kufanya kitu kama hicho. Nirafiki yangu na tumeshirikiana katika mambo mengi sana. Hawezi kufanya jambo kama hilo”

“Ni kweli muheshimiwa. Mimi ndio niliye kutorosha kutoka hospitali ya muhimbili mara baada ya makamu wa raisi kumtuma dokta ili akuchome sindano ya sumu ili ufie usingizini.”

“Niliye agizwa kutekeleza jambo hilo ni mimi hapa muheshimiwa. Ila nilishindwa kutekeleza hilo jambo na aliniahidi kunipa pesa milioni mia moja pamoja na kunipandisha cheo”

“Nilionyeshwa maono juu ya kifo chako muheshimiwa ndio maana nilimshikirisha ndugu yangu ili tuweze kukuokoa kutoka katika janga hilo”

Raisi Mtenzi akajikuta akikaa kwenye moja wapo ya sofa huku akiwatazama watu hao walipo ndani ya sebleni hiyo.

“Kwa nini alihitaji kuniua”

“Alihitaji madaraka ya uraisi na aliagiza watu wake wakutafute na endapo wata kupata basi wakuue”

“Karata una amini maneno yao hawa watu?”

“Ndio muheshimiwa. Ushahidi huu hapa”

RPC Karata akatoa simu yake mfukoni na kumuwekea raisi Mtenzi mazungumzo ya mwisho ya mlinzi wa karibu wa makamu wa raisi, akikiri kwamba makamu wa raisi alihitaji kumuua raisi Mtenzi.

“Mshenzi sana huyu”

Raisi Mtenzi alizungumza kwa hasira.

“Nahitaji kurudi ikulu sasa hivi”

“Sawa muheshimiwa. Nime kuja na vijana wa ulinzi nina imani kwamba tuta imarisha ulinzi”

“Ila nahitaji kujua ni nani ambaye amehusika katika kumuua makamu wa raisi”

“Ni mimi hapa baba”

Jery alizungumza kwa sauti ya upole huku akimtazama baba yake.

“Nini?”

“Ni mimi hapa baba.”

Jery aliendelea kusisitiza na kuwafanya watu wote ndani hapo kushangaa.

“Hivi una tambua ni jambo gani ume lifanya wewe?”

Raisi Mtenzi alizungumza kwa kufoka sana.

“Nimefanya kwa ajili ya familia yangu. Kukulinda wewe na mimi pia, alihitaji kunia alitaka kukuua nini ulihisi mimi nita fanya. Ulishitaji nisubirie aniue au akuue kabisa ndio nilipize kisasi”

Jery alizungumza kwa kufoka huku akimkazia macho baba yake.

“Chunga kinywa chako Jery. Tambua una zungumza na baba yako na sio mke wako umenielewa?”

“Nisamehe kwa kufoka ila nimefanya kile nilicho ona ni jambo jema kwa ajili ya familia yangu”

Jery alizungumza kwa sauti ya upole na kumfanya raisi Mtenzi kuwatazama watu wote waliomo ndani hapo.

“Nina waomba siri hii isiweze kutoka.”

Raisi Mtenzi alizungumza kwa sauti ya hekima.

“Haito weza kutoka muheshimiwa”

“Samahani muheshimiwa. Kabla huja rudi Ikulu nina kuomba uweze kula chakula nilicho kuandalia”

“Sawa”

Josephine akamletea raisi Mtenzi chakula hicho na taratibu akaanza kula.

“Mmmmm ni kitamu”

“Nashukuru”

“Nina kumbuka mama yangu ndio alikuwa akinipikia hichi chakula”

Josephine akatabasamu kwa furaha. Raisi Mtenzi akaendelea kula chakula hicho ambacho ni mchanganyiko wa viazi lilivyo pondwa, ndizo zilizo pondwa pamoja na nyama ya kusaga.

“Uliniambia una itwa nani binti?”

“Josephine”

“Una fanya kazi gani?”

“Mimi ni mtu ambaye nime barikiwa kupewa uwezo wa kuona mambo yajayo na ambayo yamefichika”

“Mambo yajayo?”

“Ndio”

“Moja wapo ni lipi?”

“Mimi na ndugu yangu pamoja na rafiki yetu mmoja ndio tulikuwa ni watu tulio sambaza habari kwenye mitandao ya kijamii kwamba watu waondoke jiji la Dar es Salaam kwa maana harusi ya mwanao ni batili”

“Ahaa sasa nime pata picha kumbe ndio nyinyi?”

“Ndio muheshimiwa ila tusamehe kwa hilo kwa maana tume fanya hivyo ili kuyaokoa maisha ya watu”

“Sasa ni kwa nini musinge kuja ikulu na kutupa taarifa hiyo?”

“Tusinge amininika muheshimiwa na wala tusinge pata nafasi hiyo kwako”

“Tuyaacha hayo ila niwashukuru sana kwa kunisaidia kutoka mikononi mwa mtu ambaye alinigeuka”

“Tuna shukuru pia muheshimiwa”

“Pia muheshimiwa hawa ndio waliweza kutuonyesha ni sehemu gania mbayo ulifukiwa na kifusi na wanajeshi wakakuokoa”

RPC Karata alizungumza.

“Ahaa okay nina shukuru sana. Ngoja niende ikulu alafu nita waandalia siku ya kukutana nanyi”

“Sawa muheshimiwa”

Magreth alijibu huku akiwa amejawa na furaha. Raisi Jery akamaliza kupata chakula hicho kilicho mpa nguvu mwili wake. Akaaga na akaondoka nyumbani hapo kwa Magreth akiwa ameongozana na RPC Karata, Jery pamoja na dokta Masawe.

“Kweli Mungu ni mwema”

“Ni kweli, Jose una weza kuomba na kujua ni nani ambaye eme husika na matatizo haya yote kuanzia milipuko hadi kufa kwa makamu wa raisi?”

“Muda ukifika Mungu mwenyewe ata nionyesha”

“Sawa”

“Ahaa samahani Josephine tuna weza kuzungumza”

Juma alizungumza kwa sauti ya upole na kumfanya Magreth kuwatazama kwa sekunde kisha akaelekea chumbani kwake ili kuwapa uhuru wapendanao hao kuzungumza mambo yao ya kimahusiano.

***

Wanajeshi wote walipo katika geti la kuingia ikulu, walijikuta wakishangaa sana kumuona raisi Mtenzi akiwa ndani ya gari la RPC Karata. Wakapiga saluti na geti likafunguliwa haraka haraka. Mara baada ya gari kusimama, RPC Karata akamgeukia raisi Mtenzi aliye kaa siti ya nyuma pamoja na mwanaye Jery na dokta Masawe.

“Sijajua kama waandishi wa habari wapo au wamesha ondoka muheshimiwa. Ila kama ina weza nina kuomba uweze kusubiria ndani ya gari”

“Hakuna shaka kwa wao kunionna kwa maana mimi ndio raisi wao”

“Ila baba ulivyo vaa hayo mavazi ya hospitali sio muonekano mzuri”

“Hakuna shaka mwanangu”

Raisi Mtenzi akashuka kwenye gari na kumfanya kila mtu kushangaa. Walinzi wake wakapiga saluti huku wafanyakazi wengine wa ikulu wakisalimia kwa furaha sana.

“Karibu sana muheshimiwa”

“Nina shukuru”

Raisi Mtenzi moja kwa moja akapitiliza hadi ofisini kwake na kumkuta waziri mkuu akiwa na mkuu wa mkoa wa kizungumza.

“Muheshimiwa”

Walistuka sana mara baada ya kumuona. Wakasimama na kumsalimia kwa heshimwa, raisi Mtenzi akakitazama kiti chake, kisha akazitazama picha za familia yake hususani picha ya mke wake. Raisi Mtenzi alijikuta machozi yakimwagika huku akiwa ameishika picha ya mke wake, iliyopo katika frame nzuri.

“Nahitaji viongozi wote wa ngazi za juu za usalama waweze kufika hapa ndani ya nusu saa”

“Sawa muheshimiwa hadi wa mkoani?”

“Wa mkoani wajulisheni kwamba tuta zungumza nao kupitia oline”

“Sawa muheshimiwa”

Raisi Mtenzi mara baada ya kumuachia maagizo hayo waziri mkuu akatoka ofisini hapo na kuelekea katika nyumba anayo ishi ndani ya Ikulu. Akaingia chumbani kwake, picha za mke wake pamoja na yeye zikamfanya azidi kulia kwa uchungu.

‘Lazima walipe’

Raisi Mtenzi alizungumza kwa majonzi makubwa sana. Katika maisha yake yote hakuwahi kumlilia mtu aliye fariki, ila kifo cha mke wake kime kuwa ni pigo kubwa sana kwake.

‘Mimi ni raisi, nchi ina nihitaji mimi ni lazima nisimama imara’

Raisi Mtenzi aliendelea kujipa matumaini, akaingia bafuni, akaoga haraka haraka kisha akavalia suti nyeusi.

“Vipi baba una kwenda wapi?”

Jery aliuliza kwa mshangao mara baada ya kumuona baba yake akitoka chumbani kwake.

“Nina kikao”

“Je uta kwenda saa ngapi kuutazama mwili wa mama?”

“Mara baada ya kikao changu kumalizika.”

Raisi Mtenzi akatoka ndani hapo na kuelekea katika chmba cha mkutano. Akawakuta viongozi wa ngazi za juu wa vitengo vya usalama kuanzia polisi hadi wana usalam wa taifa wapo ndani ya ofisi hiyo. Walipo mikoni waliweza kushiriki kikao hicho cha dharura kupitia wawasiliano ya video call. Mara baada ya watu wote kusimama, raisi Mtenzi akawapa ishara ya kukaa.

“Nipeni ripoti hadi sasa hivi mume fikia wapi katika matatizo yaliyo tokea?”

“Muheshimiwa raisi, kundi lililo kiri kuhusika na milipuko hiyo ni Al-Shabab”

“Mume chukua maamuzi gani hadi sasa hivi?”

“Bado hatuja fanya maamuzi yoyote muheshimiwa”

“Kwa nini?”

“Hatukupata amri yoyote?”

“Makamu wa raisi alikuwa ana fanya nini kipindi chote ambacho mimi nilikuwa sipo?”

“Hatujui muheshimiwa raisi. Ila alilo lifanya ni kuruhusu wanajeshi wa Marekani kuweza kufika hapa nchini Tanzania”

“Wana fanya nini?”

“Malengo yao ni kujenga jiji hili la Dar es Saalam.”

“Pumbavu sana. Nina jeshi kubwa la kutosha na tuna jimudu kwa kila jambo. Sihitaji kuona mwanajeshi yoyote kutoka nchi yoyote ana kuja nchini kwangu kwa madai ya kujenga jiji jipya. Jenerali Marwa”

“Ndio muheshimiwa raisi”

“Mpigie simu mkuu wa wanajeshi hao wa Marekani na sasa hivi umuambie akusanye wanajeshi wake, vifaa vyao na warudi nchini kwao. Sihitaji kuwaona hapa nchini kwangu”

Amri hiyo ikamshangaza kila mtu kwa maana raisi Mtenzi ni rafiki wa karibu sana na raisi wa Marekeni na hata nchi hizo mbili zina ushirika mzuri sana baina yao ime kuwaje ana amua kuwafukuza.



“Ila samaani muheshimiwa raisi. Makamu wa raisi alisha kubaliana na serikali ya Marekani kufanya jambo hilo.”

Mkuu wa mkoa alizungumza kwa sauti ya upole huku akimtazama raisi Mtenzi usoni mwake.

“Mimi ndio nime zungumza hivyo. Mwisho wa maelezo na hakikisheni kwamba ndani ya masaa ishirini na nne wawe wamesha ondoka nchini. Mchana mwema”

Raisi Mtenzi mara baada ya kuzungumza hivyo akanyanyuka na kuondoka kwenye ukumbi huo wa mikutano. Kila kiongozi alijawa na mshangao kwa mwenendo huo wa raisi.

“Nahisi raisi hayupo sawa”

Mkuu wa mkoa alizungumza huku akiawatazama viongozi wezake.

“Hilo ni jukumu lako, wanajeshi wamekuja ndani ya mkoa wako una masaa ishirini na nne”

Waziri wa mambo ya ndani alizungumza huku akisimama na kuondoka eneo hilo.

“Nahitaji kwenda hospitalini kuuona mwili wa mke wangu”

Raisi Mtenzi alimuambia mlinzi wake.

“Sawa muheshimiwa raisi”

Raisi Mtenzi akaondoka ikulu akiwa na walinzi wake ambao wote kwa sasa ni wapya kwani wengi wa walinzi walio kuwa wana mlinda walipoteza maisha katika mlipuko wa bomu katika hoteli waliyo fikia. Madaktari hawakuamini kumuona raisi Mtenzi akifika hospitalini hapo kwani wengi wao waliweza kuamini kwamba siku aliyo tekwa ndio simu aliyo poteza maisha yake.

“Maiti ya mke wangu ipo wapi?”

“Ipo huku muheshimiwa”

Raisi Mtenzi akaongozana na dokta Emmanuel hadi katika jengo la kuifadhi waiti. Friji lililo hifadhia mwili wa mke wake likavutwa taratibu na raisi Mtenzi, akafunua shuka lililo mfunika mke wake eneo la usoni.

“Nahitaji kuwa peke yangu”

Raisi Mtenzi alizungumza, walinzi pamoja na madaktari wakatoka ndani ya chumba hicho.na kumuacha raisi Mtenzi peke yake. Machozi yakaanza kumwagika usoni mwake. Mwanamke aliye ishi naye kwa miaka mingi, na kuvumiliana kwenye shida na raha, leo hii amelala katika eneo ambalo hakutarajia kumuona akiwa hapo.

‘Nita hakikisha nina wasalaka Al-Shabab wote na kuwaangamiza mmoja baada ya mwengine’

Raisi Mtenzi alizungumza huku akimgusa mke wake kwenye paji la uso. Akajifuta machozi kisha akatoka ndani hapo.

“Nahitaji mupange maandalizi ya mazishi ya mke wangu haraka iwezekanavyo”

“Sawa muheshimiwa raisi”

“Mume sema kwamba makamu wa raisi amefariki?”

“Ndio muhshimiwa”

“Maiti yake ipo wapi?”

“Ipo huko huko mochwari muheshimiwa”

Raisi Mtenzi akasimama kwa sekunde kadhaa kisha akageuza na kurudi katika jengo hili huku akiwa ameongozana na walinzi. Akaonyeshwa maiti ya makamu wa raisi bwana Madenge.

“Tuna weza tuka toka”

Raisi Mtenzi alizungumza kwa ufupi tu kwa maana ana tambua kwamba muhusika katika kifo cha makamu wa raisi ni mwanaye Jery ila hajatambua kwamba Jery ame fanya kitu gani hadi makamu wa raisi kufariki. Raisi Mtenzi mara baada ya kuondoka hospitalini hapo akarudi ikulu na moja kwa moja akaelekea nyumbani kwake.

“Jery nahitaji kuzungumza nawe”

“Sawa baba”

Wakaka sebleni, raisi Mtenzi kabala ya kuzungumza kitu chochote akamtazama mwanaye huyo ambaye anatambua huwa hana ujasiri wa uuji.

“Una taka kuniambia wewe ndio ume husika katika kumuua makamu wa raisi?”

“Aha…ndio baba”

“Ulifanya nini na nini hadi kumuua makamu wa raisi?”

Jery akashusha pumzi kwa maana mpango mzima uliendeshw ana mke wake pamoja na baba yake mkwe.

“Ulifanya nini hadi ukafanikiwa kumuu makamu wa raisi?”

“Niliajiri mtu baba”

“Mtu, gani na kutoka wapi?”

“Ahaa ni professional killer kutoka Mexco”

“Ulimjuaje?”

“Ahaa…baba si una jua kwamba nime ishi Marekani kwa kipindi kirefu pia hii taaluma yangu ime nikutanisha na watu wa kila aina hivyo yeye ni mmoja wa marafiki zangu.”

“Una weza kuwasiliana naye?”

“Kwa sasa ata kuwa amesha ondoka nchini Tanzania”

Raisi Mtenzi akamkazia macho kijana wake huyo na kuhisi kuna jambo ambalo Jery ana lifahamu.

“Ulimlipa kiasi gani?”

“Dola laki tatu”

“Okay. Ila siku nyingine sinto hitaji ufanye jambo la kipumbavu kama hili ambalo lina ipelekea nchi kuingia kwenye garama za kijinga”

“Sawa baba”

“Mke wako ana litambua hili jambo?”

“Hapana”

“Yupo wapi?”

“Yupo kwao”

“Muite aje hapa ikulu. Tumesha muao na kumtolea maharia na kuanzi hivi sasa ata kuwa naa ishi hapa”

“Sawa baba”

Raisi Mtenzi akanyanyuka kabla ya kuingia chumbani kwake akageuka na kumtazama Jery.

“Nahitaji uwaite wale wasichana wawili nao waje hapa ikulu, nina mazungumzo nao”

“Leo”

“Sasa hivi”

“Sawa baba”

Raisi Mtenzi mara baada ya kuingia chumbani kwake Jery akajikuta akishusha pumzi nyingi sana kwa maana amejitahidi kumdanganya baba yake ambaye siku zote sio mtu wa kudanganyika vizuri. Jery akaanza kuwasiliana na Julieth na akamuomba waweze kufika ikulu, kisha akawasiliana na Magreth na kumueleza aweze kufika ikulu hapo.

Raisi Mtenzi akajifikiria kwa sekunde kadhaa. Kisha akanyanyua mkonga wa simu yake ya mezani na kumpigia gavana wa benki.

“Habari muheshimiwa”

“Sio salama. Nahiji munitumie benk statement za mwanangu za akaunti zake zilizopo hapa Tanzania na hata nje ya nchi muda huu”

“Sawa muheshimiwa”

“Munitumie kwenye email yangu”

“Sawa muheshimiwa”

Raisi Mtenzi hakuweza kuridhishwa kabisa na mazungumzo ya mwanaye kwa maana ana mfahamu A hadi Z.

“Baba nimesha wasilia nao”

Jery alizungumza mara baada ya kumuona baba yake akitoka ndani hapo.

“Hao wasichana wawili waambie nipo ofisini kwangu. Huyo mke wako atuandalie chakula cha usiku”

“Sawa baba ila na yeye ame poteza kaka zake wote wawili”

“Kwa hiyo?”

“Ahaa…kwa nini usiwaambie wapishi ndio waandae chakula baba”

Raisi Mtenzi akamsogelea Jery kwa ukaribu hadi sehemu alipo simama. Akamkazia macho ya ukali huku akimtazama kwa macho ya msisitizo.

“Mke wangu amefariki, ila nina endelea kufanya kazi. Yeye ni nani hadi ashindwe kufanya kazi. Muambie nina hitaji apike chakula cha usiku cha watu watano. Umenielewa?”

Raisi Mtenzi alizungumza kwa msisitizo.

“Sawa baba”

Raisi Mtenzi akaelekea chumbani kwake. Baada ya dakika arobaini Josephine na Magreth wakafika ikulu hapo. Moja kwa moja wakapelekwa ofisi kwa raisi Mtenzi. Kila mmoja akashangaa kumkuta raisi akiwa ana fanya kazi zake kama kawaida.

“Karibuni mukae”

“Tuna shukuru”

Wakaka kwenye sofa zilizop ofisini hapo.

“Nime waita hapa kwa ajili ya kuwakaribisha kwa chakula cha usiku. Pia nina hitaji kuwafahamu vizuri kwa maana kitendo cha kunitorosha hospitalini na kunihifadhi pale kwenu sio jambo la kawaida tena kufanywa na mwanamke”

“Ni kweli muheshimiwa. Ila nina omba utusamehe kwa kukiuka sheria za nchi kwa maana tulifanya hivyo kwa ajili ya kuo…..”

“Usijali Magreth. Leo nii bilia ya nyinyi kuni saidia nisinge kuwa hapa. Ehee niambie mulianza vipi?”

Josephine akaanza kuadisia kuanzia alipo onyeshwa maono ya wapi raisia alipo fukiwa. Akazidi kusonga mbele na kuonyeshwa jinsi daktari aliye tumwa alivyo hitaji kumuua. Magreth akaelezea jinsi alivyo pamabana na wanajeshi na kwakusaidia na Juma wakamtoa hospitalini hapo na kuelekea naye nyumbani kwake.

“Makamu wa raisi alisha wahi kuja pale nyumbani kipindi ulipo kuwa ume zimi na niliweza kumdanganya kwamba upo mkoani Morogoro ndio maana msako ulifanyika katika mkoa huo.”

“Mshenzi sana huyu jamaa. Sasa ana taka madaraka ikiwa nime bakisha muda miaka michache kabla ya kuachia madaraka. Si angevumilia tu”

“Kila binadamu ana tamaa yake muheshimiwa”

“Magreth ulisha wahi kupitia kwenye kitengo chochote cha usalama?”

“Hapana muheshimiwa”

“Uwezo huo ume utolea wapo?”

Magreth akamuelezea raisi Mtenzi juu ya maisha yake ya utotoni. Mafunzo aliyo pitia toka alipo kuwa mdogo na kukuzwa na mzee wa kijapani hadi kufika kuwa na uwezo huo.

“Jery acha kunitania baba ame rudi kwenye hali yake?”

Juliteh aliuliza huku akiwa na mshangao.

“Ndio na anahitaji umpikie chakula cha usiku sasa”

“Huwa ana penda kula nini?”

“Mmmm mara nyingi ana penda kula ndizi, kuku wa kuchoma, kachumbari. Ila tuta saidia kupika kwa maana ana hitaji chakula cha watu watano”

“Kuna wageni?

“Ndio”

“Sawa”

Julith na Jery wakaanz akushirikiana katika kuandaa chakula hicho cha usiku huku Julieth akiwa na shahuku ya kuhitaji kumuona baba yake mkwe huyo.

***

Kichwa kikazidi kumuua Evans kwa mawazo. Mipango yake yote ambayo aliipanga na makamu waraisi asubuhi ya siku ya leo ime vurugika kutokana na kifo chake.

“Amekufaje kufanje ikiwa nilikuwa nina zungumza naye?”

Evas alizungumza huku akiendelea kutazama televishion na habari kubwa ya leo ni kifo cha makamu wa raisi.

“Nita fanya nini?”

Evans aliendelea kujiuliza mswali ambayo hakuweza kupata jibu la haraka haraka. Akaingia mtandaoni na kuanza kutafuta makundi ya kuhalifu ambayo ana amini ana weza kupata wauaji wazuri. Evans akaangukia kwenye kundi la Al-Shabab ambalo ndio kundi analo amini lina weza kufanya jambo lolote kwa ajili ya pesa.

‘Hawa kama wameweza kulipua Dar es Salaam. Hawashindi kuwalipua kina Magreth.’

Evans akaanza kutafuta njia ambazo zina weza kumuwezesha kuwapata kundi hilo la Al-Shabab na akafanikiwa kupata jina la mmoja wa watu ambao aliwatilia mashaka kwamba ana weza akawa ana husika na upatikanaji wa kikundi hicho cha kigaidi. Akaingia kwenye akaunti ya mtu huyo katika mtandao wa Facebook na kuanza kupitia pitia akaunti ya binti huyo mwenye umri wa miaka kumi na tisha na ana jiita Baby Al.

‘Mmmmmm hapa nita kuwa nime bugi’

Evans alizungumza huku akiendelea kutazama picha za msichana huyo ambaye ana onekana ni mrembo sana. Akaingia upande wa meseji na kumtumia meji.

‘Hi’

‘Hi too’

Msichana huyo alijibu kwa uharaka sana na kumfanya Evans kupata shahuku ya kuendelea kuchati naye.

‘Am Evans From Tanzania’

‘Waoo naitwa Baby Al’

‘Una fahamu kishwahili?’

‘Ndio vizuri sana’

‘Upo nchi gani?’

‘Now nipo Zanzibar kwa mapumzoko. Ila nina ishi Paris France’

‘Naweza kuja kukuona Zanzibar’

‘Una hitaji nini?’

‘Ni mambo muhimu ambayo hatuwezi kuchati kwenye simu’

‘Nita kujulisha baada ya lisaa moja’

‘Poa’

Evans akajawa na furaha sana kwa maana anaamini kwamba mashaka yake juu ya msichana huyo yana weza kutimia kwani haja yake kubwa ni kuhakikisha kwamba ana wateketeza Magreth ili mpango wake wa kupata hadhina ambayo jini Maimuna alimueleza, ana ipata haraka iwezekanavyo. Baada ya dakika ishirini akapata ujumbe kutoka kwa Baby Al ulio mfanya atabasamu sana kwa maana ana amini mambo yana kwenda kama vile alivyo panga



‘Kama una hitaji kuonana na mimi una weza kuja Zanzibar jioni hii’

Evans aliisoma meseji hiyo huku meno yote thelathini na mbili yakiwa nje kwa furaha.

‘Ndio nina weza kuja. Acha niwahi boti ya jioni hii’

‘Fanya hivyo nita kusubiria bandarini’

Evans bila hata ya kujishauri mara mbili. Akanyanyuka kitandani na kuanza kukusanya nguo zake chache na kuziweka kwenye begi. Akaondoka hotelini kwa usafiri wa taksi huku gari lake akiliacha hotelini hapo. Akafika bandanirini na bahati nzuri akakuta boti inayo ondoka dakika kumi na tano zijazo, akakata tiketi na safari ya kuelekea Zanzibar ikaanza.

‘Nimesha panda boti’

‘Waoo, tunaweza zungumza kwa video call?’

‘Yaa’

Baby Al akapiga video call hiyo kwa kupitia messenger. Uzuri wa msiachana huyo uka mfanya Evans kuzipagawa na hata lengo lake la kuhisi kwamba binti huyo ni Al-Shabab likaanza kumtoweka akilini mwake.

“Hei Handsom mambo vipi?”

“Safi you look beutful”

“Nashukuru. Ume sema una itwa Evans”

“Yaa Evans Shika”

“Karibu sana, nimependa uni patie compy”

“Usijali nipo kwa ajili yako”

“Nashukuru, safari njema”

“Nikifika tuta wasiliana”

“Sawa”

Evans akakata simu huku furaha ikiwa ime mtawala moyoni mwake. Majira ya saa mbili usikuwa wakafika bandari ya Zanzibar. Evans akashuka kwenye boti hiyo huku akiwa ana hamu kubwa ya kukutana na binti hiyo.

‘Nime fika upo wapi?’

‘Ukitoka getini uta niona, nime valia gauni jeupe na refu’

‘Sawa’

Evans akatika getini hapo na kweli akamuona Baby Al. Wakasalimiana huku wakikumbatiana kwa furaha.

“Nika hisi una nitania kwamba una kuja ndio maana niliamua kukupigia video call”

“Mimi sio mtu wa kupenda kutania watu, huwa nafanya jambo kwa kumaanisha’

“Kweli nimea amini, karibu Zazibar”

“Nashukuru”

“Nime kuja na gari langu tuna weza kwenda nilipo liacha”

“Sawa”

Wakaelekea eneo la magesho huku wakiwa wameshikana mikono. Wakaingia kwenye gari hilo huku Evans naye akikaa siti ya pembeni. Galfa Evans akachomwa sindano ya shingo na mwanaume ambaye alikuwa amejificha siti ya nyuma.

“Ni…n….ni”

Evans hata kabla hajamalizia sentensi yake akajikuta akilala usingizi fofofo. Baby Al akawasha gari huku akimtazama kijana wake huyo na wakaondoka. Wakafika kwenye godauni moja lilipo nje ya mji, eneo ambapo ndipo makazi yake yalipo huku akiwa ana vijana wake ambao ni majasusi wa kikundi cha Al-Shabab. Wakamvua nguo zote Evans na kumkalisha kwenye kiti cha chuma ambacho kime usanishwa na nyaya za shoti.

“Hei, hei, hei”

Baby Al, alimuita Evans huku akimpiga piga mashavuni mwake. Evans akakurupuka huku macho yakimtoka.

“Nipo wapi, nipo wapi?”

“Karibu, nahitaji unijibu maswali yangu laiti ukishindwa basi uta kufa.”

Evans akajawa na mshangao mkubwa saa kwani alicho kitarajia na kukitegemea kutoka kwa binti huyo sicho anacho kiona. Mshangao uka zidi kuongezeka mara baada ya kujikuta akiwa hana hata nguo moja mwilini mwake. Baby Al, akatoa ruhusa kwa kijana wake aliye kaa na mashine maalimu ya kupiga shoti kuiwasha. Evans akaanza kutetemeshwa mwili mzima, maumivu anayo yapata yakamfanya alie kama mtoto mdogo.

“Zima”

Kijana huyo akazima.

“Wewe ni nani na kwa nini ume nitafuta inbox?”

“M…i….mi…mi naitwa Evans”

“Kwa nini unitafute inbox Facebook na ume ijuaje akaunti yangu?”

“Ni likuona tu google?”

“Ndio ukaamua kunitafuta Facebook?”

“Ndio”

Baby Al akatoa ruhusa kuwashwa kwa mashine hiyo jambo lililo mfanya Evans kuanza kutetemeshwa hadi haja ndogo ikaanza kumtoka.

“Wanaume wengi wa Tanzania muna penda sana kujipendekeza kwa wasichana muna kutana nao kwenye mitandao basi leo ndio siku yako ya mwisho kuishi duania. Washa na fikisha hadi asilimia mia”

Kijana huyo akatii amri hiyo na akawasha mashine hiyo na kuiongeza hadi asilimia mia moja, Evans hakuweza kustahimili shoti hiyo na akajikuta akipiga yowe moja na kuzimia.

***

Jery akagonga kwenye mlango wa ofisi ya baba yake na akaruhusiwa kuingia.

“Aha anime wakatisha mazungumzo yenu?”

“Hapana, vipi?”

“Chakula tayari kimesha andaliwa”

“Basi, wachukue wageni, na uende nao huko nina kuja muda si mrefu”

“Sawa”

Josephine na Magretha wakaondoka ofisini hapo na kuelekea anapo ishi raisi Mtenzi.

“Karibuni”

“Tuna shukuru”

Julieth akamkazia macho Magreth kwa maana wana uaduia wa toka muda mrefu kuanzia kipindi Magreth akiwa na mahusiano ya kimapenzi na nabii Sanga hadi wakajikuta wakimpenda mwanaume mmoja ambaye ni Evans.

“Mke wangu hawa ndio wageni wa baba”

“Ahaa…za toka jana?”

Julieth alizungumza kwa sauti ya kawaida ambayo dhairi ana onekana kuto furahishwa na ugeni huo.

“Tuna shukuru Mungu”

Josephine alizungumza kwa furaha huku wakipeana mikono.

“Karibuni”

“Shukrani sana”

Magreth na Julieth wakapeana mikono ila hawakuzungumza kitu chochote.

“Jery tuna weza kuzungumza mara moja?”

“Ndio”

Julieth na Jery wakaondoka sebelni hapo na kuingia chumbani.

“Hivi una mfahamu huyo Magreth?”

“Nimeanza kumfahamu siku tulipo mfwatilia baba, kwani ana nini?”

Julieth akashusha pumzi huku akimtazama mume wake.

“Huyu binti ni tapeli wa mapenzi”

“Una maana gani?”

“Huyu msichana alitumia kuokoka wake na kutembea na baba yangu jambo ambalo lilipelekea mafarakano mengi sana kwenye familia yetu. Kuanzia nyumba, mgahawa wake na hata gari analo tembea nalo alinunuliwa na baba yangu, kitu ambacho hata nikimuona basi moyo wangu una kuwa hauna furaha kabisa”

“Una taka kuniambia Magreth alitembea na baba mkwe?”

“Ndio, laiti kama ingekuwa sio msimamo wa mama hadi leo angekuwa na baba”

“Mmmmm sasa hayo ni matatizo ya wazazi mke wangu. Tuachana naye na isitoshe si wamesha achana?”

“Ndio ila ninapo muona basi nafsi yangu huwa ina jawa na hasira kali sana”

“Mke wangu poteza, tufungue ukurasa mwengine wa maisha, sawa mama”

“Kwa ajili yako nita jitahidi”

“Sawa mke wangu nina kupenda sana”

“Nina kupenda pia”

Jery akamnyonya Julieth lipsi zake kisha wakarudi sebleni. Hukupita muda mrefu sana raisi Boaz akafika ndani hapo.

“Nime waweka sana”

“Hapana muheshimiwa”

“Baba shikamoo”

Julieth alizungumza huku akisimama.

“Marahaba mkwe wangu. Una endeleaje?”

“Namshukuru Mungu”

“Nina imani kwamba chakula tayari”

“Ndio baba”

“Basi tujumuike tule pamoja, kwa maana nina kikaa saa nne usiku”

“Sawa”

Wakakusanyika kwenye meza ya chakula na wakaanza kula taratibu huku ukimya ukitawala katikati yao.

“Mkwe chakula chako ni kitamu sana”

“Nina shukuru baba”

Josephine akajikuta akifumba macho yake huku mapigo yake ya moyo yakimuenda kasi sana. Jambo hilo raisi Mtenzi aliweza kulifahamu kwa haraka kwa maana ana uwezo wa kumfahamu mtu mwenye mashaka.

“Jose una tatizo?”

Raisi Mtenzi aliuliza na kuwafanya watu wote kumtazama Josephine ambaye hakujibu kitu chochote zaidi ya kuendelea kuyafumba macho yake.

“Vipi ana tumuite daktari nini?”

Jery alihoji huku akiacha kula.

“Hapana”

Magreth alijibu kwa maana ana tambua kwamba Josephine akiwa katika hali kama hiyo basi kuna mambo huwa ana onyeshwa.

“Kwa nini?”

“Nahisi kuna mambo ana onyeshwa”

Watu wote wakaacha kula na kumtazama Josephine, baada ya dakika chache akafumbua macho yake huku mapigo ya moyo yakimuenda kasi sana.

“Vipo Jose kuna nini?”

Raisi Mtenzi aliuliza huku akiwa na wasiwasi mkubwa sana.

“Muheshimiwa kuna mambo mawili nime onyeshwa. Una weza kuniruhusu kuyazungumza hapa?”

Raisi Mtenzi akawatazama Jery, Magreth na Julieth.

“Ndio una weza kuzungumza au yana husu mtu mmoja?”

“Hapana yana husu nchi?”

“Zungumza tu”

“Jeshi la Marekeni lina anza kutengeneza mpango wa kukushinikiza kutengua amri yako ya kuwaondoa nchini hapa kwa ndani ya masaa ishirini na nne’

Raisi Mtenzi akastuka kidogo kwa maana mazungumzo hayo alizungumza na viongozi wa ngzi za juu katika maswala ya usalama wakiwemo wa kuu wa mikoa.

“Ume juaje kwamba nili toa tamko kama hilo?”

“Muheshimiwa kama nilivyo kuambia kwamba nina uwezo wa kuona mambo yaliyopo na yajayo”

“Sawa, ehee ni mashinikizo gani ambayo wata yato?”

“Moja wata kuambia wana katisha misaada yote wanayo ipatia nchi ya Tanzania. Pili wata hitaji kuwarudisha Watanzania wote walipo nchini Marekani kurudi nyumbani na Wamarekeni wote ambao wapo nchini Tanzania wata ondoka. Tatu wata wapa yashawishi mataifa yenye ushirika na Marekani kuto ingiza msaada wowote katika nchi ya Tanzania”

Kila mtu akastuka, raisi Mtenzi akajihisi kuishiwa na nguvu.

“Sasa ni kwa nini wana fanya hivyo ikiwa nina mamlaka ya kukubali wafanye kile walicho kiomba au?”

“Mission ya wao kuja Tanzania sio kujenga jiji la Dar es Salaam pekee bali wana hitaji kuchukua hadhina ya trillions of dollars iliyopo katika eneo la posta, chini ya ardhi.”

“Hazina! Hadhina gani?”

Raisi Mtenzi alishangaa sana.

“Eneo la Posta chini ya ardhi yake futi mia mbili kwenda chini kuna mapango ambayo yalihifadhia vito vya dhamani vilivyo kuwa vina tumiwa na wafalme wa miaka ya nyuma. Muheshimiwa hiyo hadhina endapo ita patikana kwa Wamarekani basi wana zidi kuwa matajiri mara dufu na endapo ita patikana kwa Watanzania basi tuna kwenda kuwa nchi nama moja tajiri duniania na tuta kuwa na nguvu hata ya kuwa nyamazisha hao Wamarekani”

Raisi Mtenzi akashusha pumzi huku akijiweka vizuri kwenye kiti chake.

“Una uhakika na unacho kizungumza?”

“Ndio kwenye kikao chako cha saa nne usiku unacho kwenda kuzungumza na raisi wa Marekani kwa kupitia video call basi hayo ndio mashinikozo utakayo kutana nayo”

Raisi Mtenzi akazidi kushangaa kwa maana ni watu wachache sana ambao wana fahamu kwamba ana kikao na raisi wa Marekeni majira ya saa nne usiku kwa mazungumzo ya video call.

“Je nishauri nifanye nini?

“Sija onyeshwa nini ufanye katika hayo. Il anime onyeshwa hivyo tu na endapo uta zungumza naye muombe muda wa kufikiria na wala usimuambie ni sababu gani ya wao kulazimisha wana jeshi wao wajenge jiji hili la Dar es Salaam”

“Nime kuelewa”

“Jambo la pili ni kutokana na mashambulizi yaliyo fanya na Al-Shabab.”

“Ehee?”

“Una fahamu sababu ya Al-Shabab kushambulia Tanzania?”

“Ndio ni kwa sababu tuliwashambulia, mara baada ya kuwaua wanajeshi wetu kwa mlipuko wa bomu”

“Chanzo cha mlipuko ule kwenye boti una ufahamu?”

Julieth akajikuta akikaa vizuri kwenye kiti huku akimsikiliza Josephine kwa umakini sana.

“Wali tega bomu”

“Hapana muheshimiwa. Lile bomu halikusababishwa na Al-Shabab na wala hawakuhusika kabisa katika shambulizi lile”

“Kivipi ikiwa tuliona kabisa bendera zao”

“Shambulizi lile lilisababishwa na Watanzania muheshimiwa na waliweza kuwachezea mchezo wa kuwachonganisha kati ya serikali na kundi hilo la Al-Shabab.”

Maneno ya Josephine yakaanza kumfanya Julieth mapigo yake ya moyo kuanza kumuenda kasi.

“Unataka kuniambia ni Watanzania ndio wame sababisha lile tukio!?”

Raisi Mtenzi alizungumza kwa mshangao mkubwa sana.

“Ndio muheshimiwa raisi. Kuna familia ya Kitanzania ina miliki genge kubwa la madawa ya kulevya hapa Tanzania. Walitumia mbinu hiyo ya mlipuko na waliweza kupitisha madawa hayo chini ya bahari eneo lile lile la boti muda na wakati ambapo ile boti ina lipuka na kupitia mlipuko ule waliingiza kilo nyungi sana za madawa ya kulevya hapa nchini Tanzania”

Kila mtu akashangaa, huku Julieth akianza kuhisi haja ndogo ina kwenda kumtoka kwani siri ambayo alihisi kwamba ana ifahamu baba yake na mama yake leo hii ina kwenda kuwekwa hadharani.

“Ni familia gani hiyo, hao washenzi waende kulipa kwa vifo vya watanzania na mke wangu?”

Raisi Mtenzi alizungumza kwa ukali huku akimkazia macho Josephine. Ukali wa raisi Mtenzi ukamfanya Julieth atamani ardhi ipasuke na immeze kwa maana endapo ata tajwa yeye na familia yake basi huo ndio uta kuwa mwisho wa maisha yao.



“Hiyo familia bado sijaonyeshwa muheshimiwa”

Kauli ya Josephine ikamfanya Julieth kushusha pumzi na kujikuta akimuomba Mungu wake asimuonyeshe Josephine juu ya hiyo familia kwani akionyeshwa basi wata kuwa wame kwisha.

“Muombe Mungu akuonyeshe, ni lazima walipe”

Raisi Mtenzi alizungumza kwa msisitizo.

“Ni kweli baba, hiyo familia endapo ita julikana na mimi nin aomba nishiriki katika kuwapa adhabu kwa kunivurugia harusi yangu na mke wangu hapa, au una semaje mke wangu”

“Ni kweli mume wangu”

“Yaani nikiwafahamu nita waita wananchi wote, washuhudie jisi wanavyo nyongwa hadharani hadi kufa”

“Baba hivi adhabu ya kunyonga bado ipo Tanzania?”

Jery aliuliza huku akimtazama baba yake.

“Ndio bado ipo”

“Basi ita wastahili. Hao sio watu wa zuri kabisa kwenye maisha ya hii nchi kwa ujumla.”

“Ni kweli. Josephine hakikisha kwamba una weza kuipata hiyo familia haraka ili kama ni kuishuhulikia basi niishuhulikie kisawa sawa”

“Mungu ajalie katila hilo kwa maana, Mungu muda mwengine anaweza kunionyesha maono na akaficha wahusika au muhusika kwa maana ambayo hapo baadae ina onekana. Pia muheshimiwa kiwango hicho cha madawa ya kulevya bado kupi nchini na kutomana na milipuko hii, wana tumia nafasi hiyo katika kusambaza na kuzidi kuteketea nguvu kazi ya taifa”

“Nitalifanyia kazi hilo. Kesho kama huto jali nita kuomba uweza kufika hapa ikulu, ili tuzungumze kwa kina kirefu zaidi”

“Sawa muheshimiwa”

“Mimi ngoja nika jiandae na kikao”

Raisi Mtenzi akanawa mikono yake kisha akasimama na kuondoka eneo hili.

“Josephine hicho kipawa chako ulianza kukigundua toka lini?”

Jery aliuliza swali.

“Toka nikiwa mtoto mdogo kwenye Sunday school”

“Ahaa na ume kuwa una zungumza na Mungu moja kwa moja au?”

“Hata sifahamu, ila huwa nina ona kama mkanda wa video. Kuna kipindi huwa nina onyeshwa mambo makubwa hadi nina zimia”

“Duuu ni kipawa kikubwa sana. Je mtu akikuomba umuonyeshe kinacho kwenda kutokea kwenye maisha yake je ina wezekana?”

“Ina tegemea, kuna kipindi Mungu ana nifungulia na nina ona na kuna kipindi huwa hanionyeshi au hata akionionyesha basi akiniambie nisizungumze basi siwezi kuzungumza”

“Duuu kazi kweli kweli hongera sana”

“Nashukuru, hembu tutabirie mimi na mke wangu tuta kuwa na watoto wangupi?”

Josephine akajikuta akitabasamu huku akimtazama Jery usoni mwake.

“Hilo ni jambo la nyinyi kupiga goti naa kumuomba Mungu”

“Jamani sijui muna weza kuturuhusu na kuondoka”

Magreth akaingilia mazungumzo hayo.

“Mbona mapema sana”

“Tuna mwenzetu tume muacha nyumbani kule. Hivyo kama hamuta jali nina omba tuondokea”

“Sawa”

Julieth alijibu kwa maana uwepo wa Magreth na Josephine una mchanganya sana na kumkosesha amani. Kutokana Julieth amesha zungumza Jery hakuona haja ya kubisha. Wakawasindikiza hadi nje, wakaingia kwenye gari na kuondoka eneo hilo la ikulu.

“Mume wangu nina weza kwenda nyumbani mara moja?”

“Usiku huu?”

“Ndio”

“Kufanya nini?”

“Nikachukue nguo zangu na kuzihamishia hapa kwa maana hapa ndio nyumbani?”

“Tuta kwenda kesho asubuhi. Una jua kwamba toka tufunge ndoa sija pata haki yangu”

Jery alizungumza huku akimtomasa tomasa Julieth kiono chake. Wakaingia chumbani na Jery akaanza kumnyonya Julieth shingo yake. Wingi wa mawazo ya jambo alilo lizungumza Josephine hakika lilikosesha furaha Julieth na hata kazi kitendo anacho kifanya Jery kwake hakikuwana hamasa yoyote.

“Mume wangu naweza kukuomba jambo”

Jery akaacha anacho kifanya na kumsikiliza mke wake huyo kipenzi.

“Niambie mke wangu”

“Mimi naona tusifanye kwanza hadi pale tutakapo mpumzisha mama na ndugu zangu. Kumbuka kwamba tupo katikati ya misiba na walio ondoka ni watu muhimu sana, naomba tuwape heshima na tutakapo wazika basi tuta kuwa huru kwenda sehemu yoyote tunayo hitaji mume wangu”

Julieth alizungumza kwa sauti nyororo ya iliyo jaa mahaba mengi.

“Alafu kweli, tuta kuwa hatuja wafanyia haki. Namshukuru Mungu kwa kunipatia mwanamke kama wewe ambaye una weza kukumbuja hata huzuni yangu niliyo nayo”

“Nashukuru pia mume wangu. Nina kupenda sana”

“Nina kupenda pia mke wangu”

Wakakumbatiana na Julieth akafurahia kwa maana hana hamu kabisa ya kufanya mapenzi na mtu wa pekee ambaye ana mfikiria kichwani ni Josephine na anaanza kupanga mikakati ya kumdhoohofisha kwani ana weza kuwa kikwazo kikubwa sana wa kumdhohofisha kwenye biashara ya familia yake ya madawa ya kulevya.

***

Raisi Mtenzi na washauri wake wawili wapo ndani ya ofisi yake akisubiria kuunganishwa na raisi wa Marekani, kwa ajili ya kikao hicho. Raisi Mtenzi akaendelea kuwaza ni mambo ya kushangaza ambayo Josephine ame mueleza.

‘Ni familia ya nani hiyo?’

Raisi Mtenzi ajiuliza kimoyo moyo huku akiendelea kuwaza familia tajiri nchini hapa Tanzania. Akazipanga familia tatu za waarafu ambao kwa sasa wana uraisi wa Tanzania.

‘Hawa washenzi watoto wao wana ozea jela au wame rudi kwenye hii biashara hiyo?’

Raisi Mtenzi alizidi kuzichanganua familia hizoa mbazo kila familia kijana wake yupo jela kutokana na makosa ya kukamatwa na madawa ya kulevya.

‘Ni lazima nizifwatilie kwa umakini na endapo nita zikamata basi nita hakikisha wana isoma namba’

Raisi Mtenzi aliendelea kujishauri.

“Muheshimiwa tayari raisi yupo online”

Sekretari alizungumza, kisha akaiwasha tv iliyopo ofisini hapo huku ikiwa ime unganishwa kamera.

“Muheshimiwa raisi habari za masiku”

“Nina mshukuru sana Mungu nipo hai”

“Pole sana kwa matatizo yaliyo kutokea. Mimi na serikali yangu tuna wapa pole kwa tatizo hilo lililo tokea”

“Tuna shukuru”

“Muheshimiwa raisi nime pata habari kutoka kwa wanajeshi wangu. Ume toa amri ya kuondoka nchini mwako ndani ya masaa ishirini na nne, ni kwa nini ume fanya hivyo?”

“Kwa maana sihitaji huduma yao. Muheshimiwa raisi, nina imani kwamba makamu wangu wa raisi aliweza kufanya makosa katika kuwakubalia kuja nchini kwangu. Kipindi kama nchi ni kipindi cha Watanzania kushikamana kwa pamoja na kuhakikisha kwamba tuna ijenge Tanzania yetu iliyo mpya. Sidhani kama Marekani ikishambuliwa una weza kuwaita mataifa mengine kukusaidia.”

Raisi Mtenzi alizungumza kwa kujiamini huku wakitazamana na raisi huyo wa Marekani.

“Sababu zako hazina mashiko, sisi tumetoa wanajeshi kwa ajili ya kuwasaidia”

“Samahani muheshimiwa hatuhitaji msaada wa taifa jengine”

“Ohoo kumbe ni hivyo?”

“Ndio”

“Basi ndani ya masaa ishirini na nne, nita hakikisha nina sitisha misaada yote ambayo ina kuja nchini kwako na nita hakikisha kwamba Watanzania wote walipo nchini Marekani wana rudishwa ndani ya masaa hayo na Wamarekani wote ambao wapo nchini kwako, wana rudi nyumbani. Una masaa ishirini nne ya kuweza kuamua kusitisha mgogoro huu na kumbuka washirika wote wanao kusaidia kupitia mimi, nita sitisha. Usiku mwema muheshimiwa raisi”

Mawasiliano hayo yakaishia hapo na kumfanya raisi Mtenzi kuwageukia washauri wake huku akianza kuamini kwamba kile alicho ambiwa Josephine ndio hichi kime tokea.

“Yule binti ana kipawa cha ajabu sana”

“Samahani muheshimiwa una zungumzia nini?”

“Ahaahh hapana. Ehee niambie tuna fanya nini?”

“Muheshimiwa kwa nini usiwaruhusu waendelee na ujenzi wa hili jiji?”

“Bure bure?”

“Ndio muheshimiwa si wame toa msaada kwetu baada ya matatizo. Kumbuka jeshi letu lina tegeemea program nyingi za kijeshi kutoka kwa Wamarekani, ikiwemo ndege za kivita, vifaru”

“Kuna nchi nyingi sana dunia ambazo zina uwezo wa kutengeza hivyo vifaa tunavyo vihitaji. Acha wafanye wanacho weza kwa maana nasi pia ni taifa na hatuwezi kuishi kwa kutegemea amri yao.”

“Muheshimiwa raisi kumbuka kwamba tuta tumia billions of money kwenye kulirudisha upya jiji la Dar es Salaam”

“Musijali katika hilo. Tuta rudi na kuwa zaidi ya pale. Ngoja niwaambie jambo moja, pela unapo anguka nina uhakika utakuwa una wekea umakini ni kwa nini kwamba ulianguka na ilikuwaje una anguka. Jambo la kufanya ni kuto rudia makosa ya kuanguka tena. Wamarekeni ni wajanja msaada wao hawawezi kuutoa bure. Acha waondoke nahitaji kuijenga Tanzania mpya na yakujitegeme. Usiku mwema”

Raisi Mtenzi mara baada ya kuzunguma hivyo akaondoka na kuwaacha washauri wake wakiwa wamejawa na maswali yaliyo kosa majibu kwani wana ona kabisa maamuzi ya raisi wao yana weza kumtokea puani.

***

“Ni familia gani ambayo ina husika kwenye haya majanga?”

Magreth alizungumza huku akipunga mwendo wa gari lake, akakunja kuchoto na kuanza kuitafuta njia ya kuelekea nyumbani kwake.

“Hata sijajua. Nina ona Mungu bado hajaamua kunionyesha”

“Sipati picha hiyo familia ikijulikana kwa maana nina ona ina weza kuteketezwa kwa kuchomwa moto kama wezi wa kuku”

“Yaani nina waonea huruma”

“Ila watakuwa ni washenzi sana, ina wezekanaje waweke maslahi ya familia zao mbele kuliko nchi. Wakifa poa tu kwa maana hawana faida”

“Hhahaaa”

Wakafika nyumbani na Frank akawafungulia geti na kuingia ndani.

“Naona muna nukia ikulu ikulu”

“Hahaaa acha utani wako”

“Haki ya Mungu vile Jose. Yaani una nukia ikulu ikulu”

“Ina bidi siku tumuambie raisi kwamba na wewe una taka kwenda”

“Siku nikienda nina imani kwamba mizimu ya kwetu ita fufuka kwa muda kwa maana si kwa maselfie nitakayo piga”

“Hahaaaa”

“Juma kesho pajapo majaliwa, nita hitaji twende kwenye Mgahawa tukafanye tathimini ya ajali iliiyo tokea, tujua nini tuna anza kufanya”

“Sawa bosi hakuna shaka”

Magretha akaelekea chumbani kwake.

“Vipi ume kula mpenzi wangu?”

“Yaa nime shakula, ila nime wabakishia chakua”

“Sisi tumekula madiko diko ya ikulu hapa tulipo tumeshibaje”

“Kama nawaona vile”

“Hahaaa. Leo tulale pamoja mpenzi wangu nina hamu ya kukumbatiwa na wewe”

Josephine alizungumza huku akiwa amejawa na tabasamu pana usoni mwake. Sawa hakuna shaka mama, ni wewe tu”

Josephine akambusu Juma kwenye lipsi zake kisha akaelekea chumbanik wa Magreth na kumkuta akivua nguo zake.

“Vipi?”

“Safi, leo nahitaji kulala na Juma”

“Ni wewe tu ndugu yangu furahia penzi lako”

“Nashukuru. Hivi Mage una mpango gani?”

“Mpango gani kivipi?”

“Kwenye mahusiano yako ya mapenzi?”

“Nahitaji kupata mwanaume ambaye ata tuliza akili, japo bado Evans ana nafasi kwenye moyo wangu ila siwezi kumfikiria sana kwa maana bado sijajua maisha yake ya sasa yapo vipi”

“Sawa nina kuombea kwa Mungu akupatie mwanaume mzuri na mwenye kukufaa”

“Nashukuru rafiki yangu”

Josephine akatoka ndani hapo huku akiwa amejawa na furaha. Wakaingia katika chumba alicho kuwa wame mlaza raisi Mtenzi”

“Hivi hizi mashine vipi?”

“Muwarudishie Agakhan hazina kazi tena”

Josephine alizungumza huku akimkumbatia Juma na taratibu wakaanza kunyonyana lipsi zao huku kila mmoja akimvua nguo mwenzake, moja baada ya nyingine.

***

“Mkuu nine fwatilia rekodi za kijana huyu ina onyesha sio askari wala mwanajeshi”

Baby Al, akakaipokea ipad yenye maelezo ya Evans pamoja na picha yake.

“Ana onekana ana pesa?”

“Ndio kwamaana ame nunua eneo moja kigamboni kwa pesa nyingi sana”

“Tuna ondoka naye na kueleka naye makao makuu”

“Sawa mkuu”

Baby Al, akatoka ndani ya godauni hilo. Akaingia kwenye gari, vijana wake wapatao sita nao wakaingia kwenye gari jengine pamoja na Evans ambaye wame mfunga kitambaa cheusi machoni mwake, pingu mikononi mwake na myororo miguuni mwake. Moja kwa moja wakaelekea bandanirini, wakaingia kwenye meli yao ya mizigo ambayo walikuja nayo siku kadhaa, wakitokea nchini Ufaransa. Safari ya meli hiyo kuelekea nchini Nigeria ikaanza huku Evans wakimfungia kwenye moja ya kontena ambalo halina kitu chochote.

“Mkuu sasa ni kwa nini tuna ondoka na huyu jamaa?”

Baby Al, aliulizwa na mlinzi wake.

“Nahitaji kumjua vizuri”

“Una maanisha kwamba ume mpenda?”

“Zuma hivi una hisi kwamba mimi nina moyo wa kupenda”

“Nalijua hili mkuu, ila nime shangaa ina kuwaje ume kuwa na huruma na huyu kijana ambaye ame jipendekeza kwako”

“Nina hisia kwamba ana kitu anacho kihitaji, endapo nikikifahamu basi tuta jua nini cha kufanya”

“Ila kumbuka mkuu huko tunapo kwenda ndipo yalipo maficho yetu. Una hisi muheshimiwa ana weza kufurahi juu ya ujio wa kijana huyu”

“Nina imani kwamba ata zinduka kabla hatujafika na endapo ata zinduka basi nita muhoji kwa kina na endapo nita fahamu nini ana hitaji basi tuta muua na kumtupia baharini na mwili wake utakuwa ni chakula cha samaki”

Baby Al alizungumza kwa kujiamini huku akimtazama mlinziwake huyo, ambaye ni mambo mengi ya kitatili wame fanya kwa pamoja na uzuri wake ume kuwa ndio silaga kubwa sana ya kuwaangamiza wale anao wahitaji.

Evans akakurupuka na kujikuta akiwa haoni kitu chochote, akajaribu kuichanisha mikono yake iliyo fungwa kwa nyuma akajikuta akishindwa na kuanza kubingirika bingirika hadi pambezoni mwa kontena hilo.

“Haloooooooooooooo, nipo wapi hapa”

Evana alizungumza kwa sauti ila hapakuwa na mtu aliye weza kumsikia wala kumpatia msaana kwa maana yupo ndani ya kontena ambalo lipo katikati ya makontena mengine ambayo yame pangwa vizuri kuelekea juu.



Evans akaendelea kuita hadi akajikuta akianza kulia kwa uchungu sana kwa maana giza lililopo ndani ya kotena hilo sio la kawaida kabisa.

***

“Za asubuhi baba”

Julieth alimsalimia raisi Mtenzi mara baada ya kutoka chumbani kwake majira ya saa kumi na mbili kasoro asubihi.

“Marahaba, vipi usiku wenu ume kwenda vizuri?”

“Ndio baba. Vipi wewe?”

“Nimekosa usingizi na nime shindwa kulala usiku kucha. Nina mfikiria mke wangu”

Raisi Mtenzi alizungumza kwa sauti ya upole huku akimtazama Julieth usoni mwake. Taratibu Julieth akaka kwenye sofa lililopo mbele ya raisi Mtenzi.

“Mke wangu ameondoka kwenye siku ambayo nilikuwa ina furaha sana. Sinto isahau siku ya harusi yenu kwenye maisha yangu hadi nina kufa”

Raisi Mtenzi alizungumza kwa sauti ya unyonge huku machozi yakimelnga lenga usoni mwake.

“Baba”

“Naam”

“Pole kwa kila lililo tokea, najua una pitia wakati mgumu sana, ila ina bidi kumshukuru Mungu kwa kila jambo kwa maana nasi tulikuwa tuna paswa kufa ila Mungu ame tupigania na tumeweza kupona”

“Ni kweli, nina imani kwamba Mungu ametupa nafasi hii kwa makusidi kamili”

“Ni kweli baba. Ila kwa nini usichukue likizo baba ukapumzisha kichwa kwa ajili ya kujiandaa na mazishi ya mama”

“Kweli ehee?”

“Ndio baba. Japo nchi ni muhimu kwako ila hata mama ni muhimu na yeye ndio ame kuwa ubavu wako kwenye kipindi chote cha shida na raha”

Maneno ya Julieth yakamfanya raisi Mtenzi kukubaliana na jambo hilo.

“Ila nita hitaji kufanya jambo moja ndani ya siku hizi mbili ili kuiweka nchi sawa”

“Sawa baba ila nina kuonea huruma kwa manaa hii kazi yako ni ngumu”

“Ni kweli, acha tumalize hii misiba iliyopo mbele yetu nita kupatia nafasi ya kuwa katika ofisi yangu au una majukumu mengine?”

“Hapana baba nina shukuru, nipo kwa ajili yenu, wewe na Jery”

Julieth alizungumza kwa sauti ya upole iliyo mfanya raisi Mtenzi kuzidi kumuamini Julieth na kumuona ni mwanamke sahihi kwenue familia yake.

“Nikuandalie kifungua kinywa gani baba?”

“Kahawa tu ina nitosha”

“Sawa”

Julieth akaelekea jikoni na kuandaa kahawa nzuri ambayo ana amini ita zidi kumjengea nafasi ya kupendwa na baba yake mkwe huyo.

“Kahawa yako nzuri sana”

Raisi Mtenzi alizungumza mara baada ya kupiga funda moja la kahawa hiyo.

“Nashukuru baba”

Raisi Mtenzi akajiandaa na kuelekea ofisini kwake.

‘Nafasi hii nita itumia vizuri ipasavyo’

Julieth alizungumza kimoyo moyo huku akiwa amejawa na furaha kubwa sana. Akarudi chumbani na kujilaza pembeni ya Jery ambaye bado ana koroma na usingizi. Kitu cha kwanza mara baada ya raisi Mtenzi kuingia ofisini kwake, akampigia simu Josephine.

***

Mlio wa mbali wa simu inayo ita ukamfanya Josephine kunyanyua kiwacha chake kiuvivu kutoka kifuani mwa Juma. Akaangaza ndani hapo na kuiona simu yake ikiwa mezani, akashuka taratibu huku akipiga miyayo mingi. Akaichukua simu hiyo na kutazama namba inayo mpigia, akastuka sana mara baada ya kukuta ni raisi Mtenzi ndio anaye piga. Akajiweka vizuri kisha akapokea.

“Habari muheshimiwa raisi”

“Salama, mume amkaje?”

“Tuna mshukuru Mungu muheshimiwa.”

“Pole kwa kukupigia hii alafajiri sana, nina imani kwamba utakuwa ume choka”

“Hapana muheshimiwa”

“Okay. Nahitaji uje ikulu majira ya saa nne asubuhi”

“Mimi peke yangu?”

“Yaa ikiwezekana uje peke yako”

“Sawa muheshimiwa nita fanya hivyo”

“Nikutakie asubuhi njema”

“Mawe pia muheshimiwa”

“Haya”

Simu ikakatwa na Josephine akairudisha mezani.

“Nani huyo?”

Juma aliuliza kwa sauti iliyo jaa uchovu wa usingizi.

“Ni raisi”

“Ana taka nini?”

“Ameniomba niweze kwenda ikulu majira ya saa nne”

“Kwani sasa hivi saa ngapi?”

“Saa kumi na mbili kasoro”

“Bado mapema, njoo tulale”

Josephine taratibu akapanda kitandani hapo. Akamkalia Juma kiunoni mwake, huku taratibu akikipapasa kifua cha Juma. Juma pasipo hiyana yoyote, akayakamatia makalio ya Josephine, akayanyanyua juu kidogo na kumpa nafasi nzuri jogoo wake kupumua. Alipo hakikisha kwamba Jogoo wake amesimama vizuri, taratibu akamzamisha katika kitumbua cha Josephine na kumfanya kutoa miguno ya kimahaba, iliyo zidi kumpagawisha Juma na kuuanza mtanange kama walio upiga jana usiku.

Magreth mara baada ya kuamka, akasali na kumshukuru Mungu kwa kumuasha asubuhi hiyo akiwa salama salmini. Akafanya mazoezi madogo madogo ya kuupa mwili wake nguvu kama kawaida yake, kisha akajiandaa kwa ajili ya safari ya kuelekea katika mgahawa wake. Magreth akataka kugonga mlango wa chumba cha Josephine ila alivyo sikia mguno ya kimahaba, akajikuta akiurusha chini mkono wake huo. Akapiga hatua mbili mbele kisha akarudi tena mlangoni hapo, akaanza kusikilizia jinsi Josephine anavyo burudishwa na Juma. Magreth akajikuta akianza kumeza mafumba ya mate, hamu ya kufanya mapenzi ikaanza kumtawala. Akaanza kutembea kwa kasi hadi chumbani kwake. Akavua nguo zake zote za kujilaza kitandani huku akihema sana. Taratibu akachukua simu yake na kutafuta mtandao ambao una onyesha video za ngono. Alipo upata, akatafuta video moja ambayo kwa muda huo kwake aliiona ina mfaa. Taratibu akaanza kujipapasa maziwa yake kisha mkono wake huo wa kulia akaushusha chini hadi kwenye kitumbua chake na kuanza kukifikicha kwa vidole vyake viwili.

Zoezi hilo likazidi kunoga kwa Magreth na kujikuta akiingiza vidole hivyo na kuendelea kujichezea huku kwa mara kadhaa akitazama video hiyo ya binti wa kiafrika anavyo piga mechi na kijana mwenzake wa kiafrika.

‘Ohoooo…a..aiisii….ooohooo….ooa!!”

Magreth alilalama huku akiongeza kasi ya kuchezea kitumbua chake. Haukupita muda mrefu, Magreth akafika kileleeni huku mwili mzima ukimtetemeka kwa raha ambayo ni Evans pekee ndio aliweza kuileta japo kuna kipindi nabii Sanga alikuwa akijaribu kumfikisha kileleni ila sio hadi mwisho kabisa.

“Ongeza kasi baby”

Josephine alilamama na kumfanya Juma kuzidi kuongeza mwendo huku jasho likimwagika mwili mzima.

“Nakojo*** ba…..b……yyyyyy”

Josephine naye alialama huku akijikuta aking’ata mto alio ulalia kwani mkao huo wa kubong’oa huwa ana upend asana. Juma akazisha kasi huku akikishika kiono cha Josephine, naye ndani ya muda mfupi akajikuta akiwamwaga waarabu wake weupe juu ya kiuno cha Josephine.

“Asante mume wangu”

Josephine alizungumza huku akihema sana.

“Asante nawe pia mke wangu”

“Mbona ume mwaga nje?”

“Sikujua kama una penda nikumwagie ndani”

“Napenda mume wangu. Jana usiku hukumwaga, sasa hivi pia”

“Usijali mke wangu kuanzia sasa nita kuwa nina mwaga ndani”

“Sawa, ila nashukuru sana Mume wangu. Yaani toka nitolewe usichana wangu, sijawahi kukojoleshwa, ila wewe una nikojolesha”

“Hahaa kweli?”

“Haki ya Mungu vile, yaani hapa ume nifanya nime tua mzigo mzito ambao sikujua nime bebeshwa na nani”

Josephine alizungumza kwa sauti ya maaba kana kwamba sio yule anaye funga na kuomba kwa ajili ya kumuomba Mungu.

Majira ya saa tatu wakaondoka nyumbani hapo. Wakampitisha Josephine ikulu kisha Juma na Magreth wakaelekea katika eneo ulipo Mgahawa.

“Muheshimiwa raisi Josephine yupo hapa”

Sekretari wa raisi Mtenzi alizungumza.

“Mruhusu aingie”

Josephine akaruhusiwa kuingia ofisini hapo. Wakasalimina na raisi Mtenzi kwa furaha kisha akamkaribisha kukaa kwenye sofa zilizopo eneo hilo.

“Nashukuru sana kwa kuitikia wito wangu”

“Ni jukumu langu muheshimiwa”

“Kile ulicho nieleza jana, kwa kweli kime tokea kwa asilimia mia moja. Raisi wa Marekania ameshinikiza kama vile ulivo sema na yeye ame nipa masaa ishirini na nne ya kuyafikiria tena maamuzi yangu. Hembu nishauri nifanye maamuzi gani?”

“Muheshimiwa raisi, natambua itakuwa ni jambo gumu sana kwenye kufanya maamuzi na watu wengi sana wana weza kukuona wewe ni tatizo kwa uchumi wa nchi kwa kipindi hichi. Ila ina bidi ufanye maamuzi magumu katika hilo. Acha uhusiano uvunjike, ila mali ambayo Mungu alitupa kama zawadi ibakie”

Raisi Mtenzi akatingisha kichwa ikiwa ni ishara ya kukubaliana na kile anacho kizungumza Josephine.

“Kama ya kwenda mbali kwenye hayo mazungumzo. Nahitaji kukuuliza maswali kadhaa”

“Uliza tu muheshimiwa”

“Elimu yako wewe ni kiwango gani?”

“Form Six, baada ya kumaliza nilikosa mkopo na wazazi wangu hawakuwa na pesa za kuniendeleza chuo. Hivyo nilioendelea na mambo ya kawaida, ikiwemo kuimba kwanya kwenye kanisa la nabii Sanga”

“Ohooo kumbe wewe ni muumini wa mkwe mwenzangu”

“Ndio muheshimiwa”

“Bado una imba kwaya au una fanya shuhuli gani?”

“Kwaya kwa sasa sifanyi niliacha baada ya mimi na ndugu yangu Magreth kupata ajali na nikavunjika mguu, ila nime pona sasa”

“Aisee pole sana, ilikuwa ni ajali ya nini?”

“Ajali ya gari.”

“Pole kwa hiyo upo huna kazi sasa hivi?”

“Ndio, kazi yangu ambayo nina ifanyanya kutokana na wito wa Mungu, ni maombezi pamoja na kupeleka ujumbe kwa mtu ambaye nime pewa maono yake”

“Sawa, kwani nirudie tena kukushukuru kwa kweli sina cha kukulipa katika yote ulio nifanyia. Ila nina ombi moja”

“Ombi gani muheshimiwa”

“Nina hitaji uwe chief staff wa hapa ikulu”

“Mungu wangu. Muheshimiwa hiyo mbona ni nafasi kubwa sana na uwezo wangu wa kielimu ni mdogo na wala sija wahi isoema kazi hiyo”

“Una weza ukahisi kwamba elimu yako ni ndogo. Ila una kitu kikubwa ambacho hakuna mtu yoyote humu ndani ya ikulu amekuwa nacho. Una kitu ambacho kwa elimu yangu yote nilio soma, siwezi kukipata kwa maana nime amini yale maneno ya kwenye biblia yanayo sema. Watu wangu wana teketea kwa kukosa maarifa. Laiti kama ninge pata maarifa kwenye hatua ya kwanza kabisa kwenye lile shambulizi la askari wangu, basi leo hii nchi isinge poteza watu wengi kama hivi”

Raisi Mtenzi alizungumza huku machozi yakimlenga lenga usoni mwake. Josephine akajikuta akiminya minya vidole vyake kwa maana hajawahi kumuona raisi akiwa katika hali ya huzuni kama hiyo.

“Ikulu ina hitaji mtu kama wewe. Ikulu ina hitaji mtu ambaye ana weza kutuongoza kiroho. Tafadhali Josephine nina kuomba sana ukubali ombi langu”

“Muheshimiwa nina shukuru sana kwa nafasi hiyo uliyo nipatia. Ila nina kuomba sana unipe muda nipige goti na kumuomba Mungu, endapo ata nipatia kibali basi nita ungana na wewe hapa ikulu”

Raisi Mtenzi akatabasamu kwa maana Josephine ame ana onekana sio mtu wa tamaa kwa maana laiti ingekuwa ni mtu mwengine angekubali haraka haraka hata pasipo kuangalia nafasi ya kazi hiyo ambayo ni kubwa sana kuliko hata jinsi mtu anavyo ifikiria.

***

Jery na Julieth wakafika nyumbani kwa nabii Sanga na kukuta viongozi wa kanisa pamoja na waumini wengine wakiwa wame kusanyika katika kuandaa mazishi ya watoto wawili wa nabii Sanga. Wakasalimiana na watu baadhi kisha wakaingia ndani.

“Baba yupo wapi?”

Julieth alimuuliza mfanyakazi wao wa ndani.

“Yupo gorofani”

“Sawa”

Julieth akapandisha na moja kwa moja akaelekea kilipo chumba cha wazazi wake. Akagonga na mlango ukafunguliwa na mrs Sanga.

“Shikamoo mama”

“Marahaba”

“Naweza kuingia”

“Ndio”

Julieth akaingia na kumkuta baba yake akimalizia kuzungumza na simu.

“Baba shikamoo”

“Marahaba. Ehee vipi usiku wako wa kwanza na mume wako ume kwendaje?”

“Salama tu baba. Ila kuna tatizo”

“Tatizo!! Tatizo gani?”

Nabii Sanga aliuliza huku akiwa na mshangoa.

“Muna mjua yule Josephine ambaye ana maono maono gani sijui huko?”

“Ndio, ame fanya nini tena?”

Mrs Sanga aliuliza.

“Jana walialikwa chakula cha usiku ikulu na raisi, yeye pamoja na yule mpuuzi Magreth. Tukiwa katikati ya chakula, sijui akaoteshwa au ndio kuonyeshwa. Hamuwezi amini alainza kusimulia tukio niliko lifanya juu ya kupitisha madawa siku ile hadi mwisho na akasema kuna familia ambayo ina jihusisha na biashara hiyo na milipuko yote iliyo tokea hapa Dar”

“Mungu wangu alitutaja?”

Mrs Sanga aliulia huku akiwa na wasiwasi.

“Jambo la kumshukuru Mungu ni kwamba hakututaja na hakuonyesha hiyo familia. Baba tuna fanyaje tupo kwenye tatizo na mbaya zaidi yupo karibu sana na raisin a sipati picha siku tukitajwa hizi nyuso zetu sisi tuta zificha wapi sisia baba”

Nabii Sanga akajikuta akikaa kitandani huku akishusha pumzi nyingi sana kwani taarifa hiyo ime mkata maini, kwani ana utambua vizuri sana uwezo wa Josephine na endapo akionyeshwa juu ya mauvo ya familia yake basi ata yaweka hadharani pasipo kuongopea wa kuficha jambo lolote lile.



“Huko tunapo kwenda sio pazuri”

Nabii Sanga alizungumza huku akikaa akimtazama Julieth pamoja na mke wake.

“Sasa tuna fanyaje mume wangu”

“Hata sijui ni nini tufanye”

“Ina bidi tumuue baba”

Nabii Sanga na mke wake wakamtazama Julieth aliye toa pendekezo hilo.

“Una hisi ni rahisi kama hivyo unavyo zungumza?”

Nabii Sanga alizungumza huku akimtazama Julieth usoni mwake.

“Yule msichana ana tumiwa na Mungu wa kweli na kitu ambacho hamukijua hata mpango mbaya mukiupanga dhini yake basi ana weza kuujua na ana weza kuuepuka”

Nabii Sanga aliendelea kutolea msisitizo juu ya sifa ya Josephine.

“Sasa baba tukimuacha huoni kama ana weza kutudhuru?”

“Ni heri kukaa kimya na usubiria ni nini kitakacho tokea, kuliko tukaanza kumuwinda alafu akafunguka kwa kila jambo kwa mkwe wako. Nina uhakika tuta kufa kifo katika wakati ambao bado hatujauhitaji”

“Kwa hiyo baba una shauri kwamba tuweze kumuacha?”

“Tena wala usimfikirie kabisa kwenye mipango mibaya”

“Mmmmm sawa”

Julieth alikubali kishingo upande.

“Alafu baba mkwe ameniambia kwamba ana hitaji kunipatia nafasi ikuli”

“Kweli?”

Mrs Sanga aliuliza huku akiwa amejawa na furaha kubwa sana.

“Ndio mama”

“Mpango wetu una kwenda kama vile tulivyo panga. Ni wakati wako wa kuwa karibu sana na raisi ili kufahamu hatua na miendendo yote ya jinsi nchi inavyo kwenda kwenye swala zima la kupambana na madawa ya kulevya”

“Sawa baba. Nime kuja na Jery”

“Ohoo acha nikamsalimie”

NabiI Sanga akatoka ndani hapo na kuwaacha Julieth na mama yake.

***

“Bosi una onaje tuka hamisha eneo la mgahawa huu, tukajenga sehemu nyingia ambayo itakuwa na nafasi kubwa sana ya wateja wetu kujipatia huduma”

“Hilo nilikuwwa nina lifikiria sana Juma. Tuanze kufanya mchakato wa kupata eneo jipya tena kabla ya huu mji haujatengenezwa na kurudi kwenye ubora wake”

“Sawa bosi nita litilia mkazo hilo nalo”

Simu ya Magreth ikaanza kuita, akaitoa mfukoni na kukuta nin namba ya Josephine.

“Niambie”

“Mupo wapi?”

“Eneo la mgahawa vipi umesha maliza mazungumzo na raisi?”

“Ndio basi nisubirini hapo”

“Sawa”

Magreth akakata simu yake na wakaendela kutazama uharibifu ulio tokea eneo hilo. Baada ya dakika ishirini Josephine akashushuka kwene gari la secrety service.

“Duu ume pewa usafiri wa gari za raisi?”

“Yaani wee acha tu ndugu yangu. Muheshimiwa ame niomba niwe katika nafasi ambayo kwa kweli nina hofu nayo”

“Nafasi gani?”

Juma aliuliza huku akimtazama Josephine usoni mwake.

“Nita wambia tukiwa nyumbani. Kaka zangu nina shukuru muna weza kwenda tu”

Josephine aliwaruhusu walinzi hao wawili kuondoka. Baada ya walinzi hao kuondoka wakatafuta eneo na kukaa.

“Eheee tuambie kwa maana una onekana una furaha sana”

“Raisi ana hitaji niwe chife staff wake”

“Chief staff ndio kazi gani?”

Juma aliuliza huku akiwa amejawa na mshangao.

“Ni kazi ya kumsaidia raisi, kumshauri na kuwa mtunza siri wa ofisi yake na pia kuwa kiongozi wa wafanyakazi wengine ndani ya ikulu”

Magreth alimjibu Juma kwa maana hakuwa na uelewa katika kazi hiyo.

“Sasa Josephine hiyo ni kazi nzuri sana”

Magreth alizungumza.

“Ila bado sija pata kibali kutoka kwa Mungu. Acha kwanza nimuombe Mungu ili niipate nafasi hiyo”

Josephine alijibu kwa upole.

“Sawa ni jambo zuri”

Juma alijibu kwa unyonge.

“Ila mpenzi wangu mbona una onekana kama kuwa mnyonge”

“Kazi ambayo una kwenda kuifanya si ita kuweka mbali na mimi kwa maana hatuto kuwa tuna onana”

“Sidhani na isitoshe kama Mungu ata kubali niiifanye hiyo kazi basi nita kuwa nina kualika kuja ikulu”

“Ina ruhusiwa?”

“Ndio”

“Mmmm sawa”

Juma hakuonekana kuwa na furaha kabisa na taarifa hiyo japo ana jikaza kuwa na tabasamu usoni mwake. Kitu cha kwanza mara baada ya kurudi nyumbani. Josephine akajifungia ndani kwake na kuanza kumuomba Mungu aweze kumruhusu juu ya kazi anayo iendea. Mwili mzima wa Josephine ukaanza kutetemeka, mambo ambayo anaonyeshwa hakika sio madogo hadi mwishowe akajikuta akizimia.

Majira ya saa mbili usiku, Josephine akazinduka mara baada ya kuzimia kwa masaa matatu mfululizo. Akatoka ndani hapo huku akiwa na sura iliyo jaa huzuni kubwa sana.

“Vipi mbona una huzuni?”

Magreth alizungumza huku akiendelea kupija chakula cha usiku.

“Hakuna”

“Mmmmm kwema lakini?”

“Ndio”

Josephine alijibu kwa sauti ya unyonge. Magreth akazima jiko hilo la gesi kisha akamsogelea Josephine sehemu aliyo simama jikoni hapo.

“Jose mimi nina kujua wewe vizuri sana. Hembu nieleze ni kitu gani ambacho kime tokea huko?”

Magreth alizungumza kwa sauti ya upole huku akimshika Josephine mashavuni mwake.

“Nime onyeshwa mambo makubwa hadi nime zimia”

“Kumbe ulikuwa ume zimia?”

“Ndio”

“Mungu wangu. Ni mambo gani hayo?”

“Sijapewa kibali ya kuyazungumza sasa hivi. Ila nilicho kubaliwa ni kuwa karibu na raisi”

“Kuwa pembeni ya raisi una maana Mungu ame kubali uweze kuwa chief staff wa raisi?”

“Ndio”

“Waooo ni jambo zuri sana”

Magreth alizungumza huku akiwa na furaha kubwa sana, ila Josephine hakuonekana kabisa kuwa na furaha kwani hayo aliyo yaona hakika yana muogopesha na kumkosesha amani kabisa moyoni mwake.

***

Evans akatolewa kwenye kontena hilo huku akiwa amelegea mwili mzima kwani amekaa masaa mengi sana pasipo kupata chakula chochote. Moja kwa moja akapelekwa hadi katika chumba alichopo Baby Al pamoja na mlinzi wake. Evans akakalishwa kwenye kiti ambacho mbele yake kuna meza iliyo jaa vyakula vya kutosha.

“Mfungueni pingu”

Evans akafunguliwa pingu na kisha walinzi walio mleta wakatoka ndani hapo na kumuacha na bosi wao pamoja na mlinzi wa bosi wao.

“Una weza kula”

Baby Al alizungumza huku akimtazama Evans aliye legea. Evans hakutaka hata kujishauri mara mbili, akaanza kula vipande vya mishkaki huku huku akifakamia na juisi ya chungwa. Baby Al, akatabasamu na taratibu akaendelea kula huku mlinzi wake akiwa eme simama kwenye moja ya kona ya chumba hicho. Evans akaendelea kufakamia vyakula hivyo hadi alipo jijsi kushiba, ndipo akapata nafasi nzuri ya kumtazama Baby Al.

“Una jisikiaje?”

Baby ali alizungumza huku akimtazama Evans usoni mwake.

“Nipo wapi hapa”

“Upo sehemu isiyo na jina”

“Una maanisha nini?”

“Upo sehemu ambayo ina jina”

Baby Al alizungumza huku akinyoosha mkono wake wa kulia, mlinzi wake akachomoa bastola yake kiunoni na kumkabidhi bosi wake huyo. Baby Al akaikoki bastola hiyo na kumyooshea Evans aliye anza kutetemeka mwili mzima.

“Najua ume shiba sasa. Hata ukifa basi uta kufa ukiwa ume shiba si ndio”

“Na….na….a..kw……a….aa….ni”

Evans alibabaika, imani yote kwa mwanamke huyo ime muisha.

“Una sema nini?”

“Kwa….ni…ni una taka kuniua?”

“Kwa sababu huna faida”

Evans machozi yakaanza kumwagika, ujanja wote ume muisha usoni mwake.

“Kwa nini ulinitafuta”

“Kwa sababu nina hitaji msaada”

“Msaada gani?”

“Nina hitaji kuwaua watu fulani ila sina uwezo wa kufanya hivyo ila nina pesa za kuwalipa”

“Pesa za kutulipa, kwani ume ambia sisi ni wauaji?”

Evans akashusha pumzi huku akimtazama Baby Al.

“Ipo hivi, kuna watu wa ngazi za juu mmoja wapo akiwa ni mtoto wa raisi wa nchini Tanzania Jery Mtenzi pamoja na mtoto wa nabii Sanga. Nina hitaji muweze kuwaangamiza, nilikuwa nina tafuta kikundi cha kigaidi, hivyo katika kupeleleza kwangu nikagundua kwamba wewe una kamuunganiko na kundi la Al-Shabab, hivyo nilianza kukufwatilia japo sio rahisi kwa mtu kuweza kujua kama wewe una husika na kundi hilo. Tuliwasiliana ili muweze kunisaidia, nipo tayari kuwalipa kiasi chochote munacho hitaji”

“Wewe ni askari?”

“Mimi sio askari, ni mtu wa kawaida sana ambaye nina hitaji kulipiza kisasi changu kwa njia hiyo”

Baby Al wakatazamana na mlinzi wake.

“Wewe una kiasi gani cha kutulipa?”

“Sijajua kutokana na kazi ambayo sio hiyo tu kuna wengine wawili nao wana paswa kufa”

“Wangapi?”

“Wawili ambao mmoja wao ana itwa Josephine na mwengine anaitwa Magreth.”

“Mkuu tuna weza kuzungumza?”

“Ndio”

Baby Al akatoka nje ya chumb hicho na mlinzi wake huyo.

“Asije akawa ana tuingiza mitegoni huyu jamaa”

“Kumbuka upo na mtu mwenye akili. Bado hatupo mbali sana na Tanzania. Tuna weza kutuma vijana wawili wakaenda kuifanya kazi hiyo mara baada ya malipo”

“Sasa uta muachia?”

“Hapana, tuta muachia mara baada ya kazi hiyo kuisha na ikiwezekana tuna weza kumuua kabisa”

“Sawa”

“Ila kama hii kazi tuta ifanya basi tuifanye hapa hapa na isihusike na kikundi chetu kama unavyo fahamu balaa walilo lifanya nchini Tanzania”

“Ni kweli muheshimiwa”

Baada ya kujadiliana hivyo wakarudi ndani na Baby Al akakaa kwenye kiti chake.

“Ehee malipo yetu tuna yapataje?”

“Kama muna akaunti ba benki basi nina waingizia hicho kiasi”

“Niletee laptop”

Mlinzi wa Baby Al akatoka ndani hapo na baada ya muda akarudi akiwa na laptop iliyo ndani ya brufcase ngumu.

“Kila mtu mmoja tuta muua kwa dola laki mbili na nusu. Kama upo tayari pesa tuingizie sasa hivi”

Baby Al alizungumza kisha akamsogezea Evans laptop hiyo.

“Sasa mukishindwa kuwaua je pesa yangu ita rudije”

“Tambua kwamba hadi kutupata sisi ni kutokana na sifa ulizo ziona kwetu. Kama huijati kufanya bishara nasi basi ni heri tuka kuua na kuutupa mwili wako baharini”

Baby Al alizungumza kwa msisitizo na kubwa na kumfanya Evans kuitazama laptop hiyo, akamtupia jicho jaama aliye kaa pembeni hapo na ana onekana ni mtu asiye na masihara kabisa.

“Kwa hiyo niingize kiasi hicho chote”

“Ndio”

Evans akaanza utaratibu wa kuhamisha pesa kutoka kwenye akaunti yake na kuelekea kwenye akaunti aliyo kabidhiwa na Baby Al ambaye alikuwa haamini kama Evans ana kiasi cha pesa hizo. Baada ya hatua hiyo kukamilika, Baby Al, akajikuta akitawaliwa na furaha kubwa sana na hata wazo la kuumuua Evans likaanza kuyayuka kichwani mwake taratibu.

“Picha za hao una hitaji tuwaue”

Evans akaingia kwenye mtandoa, akaitafuta picha ya Jery ambayo ime ambatana na picha ya Julieth. Akaitafuta picha ya Josephine na Magreth na akafanikiwa kuzipata.

“Mkuu nita lishuhulikia hili”

Mlinzi wa Baby Al alizungumza huku akizitazama picha hizo.

“Una uhakika Zuma una weza kulifanya hilo?”

“Ndio mkuu niamini”

“Basi ondoka na boti usiku huu kurudi nchini Tanzania, tuta tia nanga hapa”

“Sawa muheshimiwa. Huyu naye je?”

“Niachie hapa”

Zuma akamtazama Baby Al kisha akatoka ndani hapo, akafanya maandalizi yote ya safari ya kurudi nchini Tanzania kisha, akaingia kwenye boti ndogo yenye mashine mbili na kuondoka eneo hilo huku akiamini kwamba kazi ya kuwaua watu alio onyeshwa ita kuwa ni nyepesi sana kwake.

***

Kila muda macho ya Magret yapo kwa Josephine ambaye ana onekana ana mawazo. Hata chakula hicho wanacho kula hapo mezani ana onekana kuto kufurahishwa nacho. Akamtazama Juma ambaye kwa sasa wame amua kuishi naye kabisa hapo nyumbani, yeye yupo bize na kuendelea kushindilia vijiko vya ubwabwa samaki.

Josephine akanyanyuka na kuondoka eneo hilo huku akilengwa lengwa na machozi

“Jose vipi?”

Juma aliuliza huku akimtazama Josephine anaye elekea mlango wa kutokea mbele. Magreth kwa haraka akacha kula na kutoka nje. Juma akatoka kutoka ila Magreth akamzuia kwa ishara asiweze kuondoka eneo hilo.

“Jose Jose”

Magreth aliita huku akimkimbilia Josephine anaye toka nje ya geti. Akamkuta Josephine akiwa amesimama pembeni ya geti huku akilia kwa uchungu.

“Jose kuna nini?”

Magreth aliuliza kwa sauti ya upole huku akimtazama Josephine usoni mwake. Taratibu Josephine akaka chini na kumlazimu Magreth naye kukaa chini.

“Jose niambiea rafiki yangu ni kitu gani kinacho kusumbua. Una onekana huna furaha kabisa”

“Mage”

“Beee”

“Nakupenda sana rafiki yangu”

“Hata mimi pia nina kupenda sana Josephine. Niambie una tatizo gani”

Josephine akajifuta machozi yake usoni na kumtazama Magreth.

“Katika maono ya leo niliyo onyeshwa, nime onyeshwa mambo ya kutisha sana. Nina shindwa kuyahimili kifuani mwangu, nikiyakumbuka nina hisi kuchanganyikiwa na uchungu mwingi sana rafiki yangu.”

Josephine alizungumza kwa uchungu sana huku akiendelea kulia na kumfanya Magreth kuanza kujawa na wasiwasi kwa maana hali kama hiyo hajawahi kuina kwa rafiki yake huyo.




ITAENDELEA



0 comments:

Post a Comment

BLOG