Search This Blog

Wednesday, November 18, 2020

MKE WA RAISI (PRESIDENT‘S WIFE) SEHEMU YA 10 MWISHO

 

 


 MKE WA RAISI (PRESIDENT‘S WIFE)

WRITER…………………………………………EDDAZARIA G.MSULWA
WEBSITE………………………………………… www.storyzaeddytz.com
CONTACT……………………………………….. 0657072588/0768516188
AGE……………..18+ 

SEHEMU YA 10 KATI YA 10

 


Majira ya saa moja usiku Adrus akaondoka katika hoteli hiyo na kuelekea, ikulu. Majira ya saa tatu kasoro akafika ikulu, akawasiliana na Eddy na akatoa ruhusa ya Adrus kuingia ikulu, kwa maana hana kitambulisho chochote cha kumuonyesha kwamba yeye ni nani. Moja kwa moja akaelekea ofisi kwa raisi na kuwakuta wakimsubiria.

“Karibu”

Rahab alizungumza kwa kujishuku kwa mana anafahamu mambo ambayo aliwahi kumfanyia Adrus.

“Nashukuru muheshimiwa”

“Sasa dogo, tunahitaji kuelekea Morogoro, katika kijiji kimoja, Rahab ndio anakifahamu”

“Sawa mimi nipo tayari sasa tunatokaje ikiwa walinzi wapo hadi hapo mlangoni?”

“Cha kufanya hivi sasa, sisi tutatumia njia za chini za dharura. Tutakwenda kutekea pale Posta eneo lile lenye sanamu kuna uwazi ambao tunaweza kutoka, sasa inabidi wewe uende pale ukatusubirie”

“Sawa muheshimiwa, ila munaweza kuniambia japo kwa ufupi ni kwa nini munahitaji kutoroka ikulu pasipo mtu wa aina yoyote kufahamu?”

“Kuna mzee mmoja ambaye ni rafiki yanguw a siku nyingi, ninahitaji kwenda kuona naye”

“Sawa, inabidi niweze kupata silaha”

“Sisi tutakuja nazo”

“Sawa”

Adrus akatoka ofisini humo na kuwaacha Eddy na Rahab.

“Twende chumbani kwangu”

“Sasa hivi?”

“Ndio, huko ndio kuna njia ya kutoka hapa ikulu pasipo walinzi wetu kufahamu kitu chochote”

Eddy hakuhitaji kukataa, moja kwa moja wakaelekea katika chumba cha Rahab. Rahab akafungua kabati lake la kuhifadhia silaha, wakachagua bastola sita pamoja na magazine zaidi ya thelathini zilizo jaa risasi, wakaziweka katika moja ya begi la mgongoni. Rahab akavua nguo zake na kuvaa suruali pamoja na tisheti, akachukua kofia na kuivaa.

“Hapo upo sawa?”

“Yaaa”

“Una buti zozote uvae hivyo vijiraba siviamini sana”

“Kuan hizi travolta hapa naweza kuzivaa?”

“Yaa zivae”

Rahab akabadilisha viatu kama alivyo elezwa na Eddy.

“Wewe je?”

“Mimi hivi hivi na suti yangu nipo poa”

“Jeraha hilo la mguuni vipi?”

“Maumivu ni kwa mbali sana, ila nipo poa”

“Eddy”

“Ndio”

“Najua yote haya unafanya kwa ajili yangu, ila ninakuomba usichukie kwa kile ambacho utakwenda kukisikia kwa huyo mzee”

“Siwezi kukichukia?”

“Kweli?”

“Ndio”

Taratibu Rahab akamsogelea Eddy na kuanza kumnyonya lisp zake kwa hisia kali sana huku machozi yakimbujika kwani moyoni mwake bado anasikia msukumo unao muonyesha kwamba sikuu hii ya leo itakuwa mbaya sana kwenye maisha yake.



Wakaachiana taratibu, Eddy kwa viganja vyake akamfuta Rahab machozi yanayo mwagika.

“Jikaze nitakulinda kwa maisha yangu yote sawa Rahab”

“Nashukuru kwa kusikia hivyo”

“Ni muda wa kuondoka sasa”

Eddy alizungumza hukua kilivaa begi hilo lililo jaa magazine zilizo jaa risasi za kutosha. Rahab akapiga hatua hadi kwenye mlango wa siri ambao unamsaidia raisi kutoroka ndani ya ikulu endapo kunatokea dharura ya aina yoyote. Rahab akamtazama Eddy kisha akivua saa yake iliyopo mkononi mwake, kwani ina GPRS, ambayo inawawezesha walinzi wake kuweza kufahamu kila sehemu ambayo raisi anakwenda.

“Sihitaji walinzi waweze kufahamu hili swala kama ninatoka hapa ikulu”

“Sawa”

Wakaingia katika mlango huo wa siri, na wakachukua tochi maalumu ambazo hukaa pembezoni mwa mlango huo ambapo ndani ya kuna giza nene sana ambalo si rahisi kuona mbele pasipo kutumia mwanga wa aina yoyote basi hawawezi kupiga hata tatua mbili mbele. Eddy akamshika Rahab mkono na wakaanza kutembea ndani ya njia hiyo iliyopo chini ya ardhi.

“Tunatumia muda gani kutoka ndani ya hii njia?”

“Kama dakika kumi na tano hivi”

“Hii njia ulisha wahi kuipita kabla?”

“Yaa niliwahi kuipita nikiwa na marehemu mume wangu, kuna sehemu kuna njia zaidi ya nne ambazo unaweza kutokea sehemu mbalimbali katika jiji hili la Dar es Salaam”

“Okay”

“Ni hapo mbele tu tunaweza kufika katika njia hizo zilizo gawanyika”

Wakafika katika njia hizo na Rahab akamuonyesha ni njia gani ambayo wanaweza kuipita hadi wakatoka katika eneo la mwenge ambapo watakuana na Adrus ambaye tayari walisha muagiza. Ndani ya dakika kumi na nane wakawa wamefika katika eneo la Mwenge. Taratibu Eddy akawa mtu wa kwanza kupanda katika ngazi hizo za chuma kuelekea juu. Akafungua mfuniko wa chuma ambao umefunika katika sehemu hiyo, kisha taratibu akachungulia nje na kumuona Adrus akiwa amesiamam karibu kabisa na eneo hilo, akampigia mluzi kidogo na Adrus akamfwata kwa haraka.

“Hii sehemu ipo salama?”

“Ndio muheshimiwa”

Taratibu Eddy akatoka nje, kisha raisi Rahab akatoka, wakaufunika mfuniko huo na kuelekea kwenye gari pasipo watu kadhaa walipo katika eneo hilo kuweza kuelewa ni kitu gani ambacho kinaendelea. Wakaingia kwenye gari, Eddy akavua begi alilo livaa mgongoni na kutoa bastola mbili na magazine nne na kumkabidhi Ardus.

“Gari lina mafuta ya kutosha?”

“Inabidi niingie hapo sheli na kuongeza”

“Sawa”

Adrus akawasha gari na wakaondoka katika eneo hilo, wakafika katika moja ya sheli kubwa. Adrus akajaza mafuta tanki nzima ya gari kisha akabeba na mafuta ya ziada katika dungu la lita ishirini na safari ya kuelekea mkuoani Morogo ikaanza rasimi.

“Umewasiliana na mke wako?”

Rahab aliuliza kwa sauti ya upole na unyonge mwingi sana.

“Hapana”

“Kwa nini?”

“Sitaki mtu anivuruge katika hii safari ni kazi muhimu ya kiserikali na nina imani anafahamu ni majukumu gani ambayo ninatakiwa kuayafanya kama raisi wa nchi”

“Sawa”

“Adrus?”

“Ndio mkuu”

“Umefurahia mahusiano yako ya sasa na Naomi”

“Ndio muheshimiwa”

“Sawa, kitu cha muhimu kwa sasa hakikisha kwamba haendani kinyume na akairudia familia yangu sawa kwa maana kufanya hivyo mimi siwezi kumsamehe”

“Sawa muheshimiwa nina imani hato weza kufanya jambo hilo”

“Nashukuru sana”

Eddy alizungumza kwa sauti ya upole huku gari likizidi kusonga mbele.

***

K2 na Jonh pamoja na mshauri wao wakaianza safari ya kuelekea mkono Morogoro huku wakiwa na kikosi cha walinzi zaidi ya kumi na mbili ambao nao wamepanda katika magari mawili tofauti na kuliweka katikati gari walilo panda K2 na wezake.

“Una uhakika huyo mtu tunaye mfwata huko atakuwa na siri sahihi ambayo sisi inaweza kutusaidia kwa kumuanganiza raisi Rahab?”

K2 alimuuliza mshauri wa kaka yake huku akimtazama usoni mwake.

“Ndio nina uhakika wa asilimia mia moja, naamini hiyo siri itakuwa ni kubwa kiasi kwamba itatupa usihindi mkubwa sana”

“Dereva ongeza mwendo basi tuwahi kufika”

K2 alizungumza kwa msisitizo na kumfanya dereva kuongeza mwendo kasi wa gari lao.

“Ni lazima niwe raisi wa hii nchi”

John alizungumza huku akimtazama mdogowake usoni.

“Usijali kaka ni lazima tuhakikishe kile tulicho kipanga kinafanikiwa.”

“Amen”

***

“Mbona Cookie hajatoka leo ndani siku nzima?”

Phidaya alimuuliza Shamsa wakiwa katika chumba cha watoto wao wanapo walaza.

“Ameachwa”

“Ameachwa, kivipi?”

“Mpenzi wake amekutana na mwanamke mwengine ambaye alikuwa naye kwenye mahusiano kabla ya huyu na ameamua kumuacha kabisa”

“Weeee!!”

“Ndio hivyo na mama mtu amechangia kwa asilimia kubwa sana kwa mwanaye kumuacha msichana wa watu”

“Ila mbona mtoto wa watu ni mzuri sana, ana kasoro gani?”

“Ndio wanaume, wanaume siku zote sio watu wa kuwaamini”

Shamsa alizungumza kwa sauti ya upole huku akimtazama Phidaya usoni mwake.

“Masikini weee, ila alicho fanyiwa sio kitu kizuri kwa kweli”

“Ni kweli sio kitu kizuri ila ndio yaliyo tokea”

“Ngoja nikamuone, kwa maana atakuwa hajapata hata chakula na sasa ni saa tano kasoro usiki huu”

“Sawa ila natamani Adrus arudi nizungumze naye mimi kama mimi?”

“Hivi Sa Yoo na Lee Ji, toka walivyo ondoka na Eddy hawajarudi?”

“Ndio bado hawajarudi”

“Mmmm watakuwa wamekwenda wapi jamani?”

“Sijajua, ila kutokana wapo wote wanne akiwemo na Adrus nina imani kwamba watarudi salama”

“Sawa ngoja nikamuangalie huyo binti wa watu”

Phidaya katoka ndani ya chumba hicho, moja kwa moja akapitiliza hadi jikoni na kumkuta mama Adrus akiwa amekaa kwneye moja ya kiti kirefu kilchopo ndani ya chumba hicho huku akinywa pombe kali sana hadi Phidaya akastuka kidogo.

“Mama Adrus?”

“Mmmm……..”

“Vipi mbona unakunywa pombe kali kiasi hicho, hiyo pombe huwa nimezoea kumuona Eddy akinywa hii pombe”

“Hahaaa mama mtoto unahisi mimi kunywa hii pembe ni vibaya sana eheee?”

Mama Adrus alizungumza huku akicheka sana. Phidaya akaka kimya huku akimtazama Mama Adrus, akaichukua chupa hiyo ya pombe ina ya wisk iitwayo JB na kurudisha katika kabati kubwa la vinuwaji lililomo ndani ya chumba hicho cha jiko hilo la kisasa.

“Kunywa pombe kali kiasi hichi ni hatari kwa afaya yako”

Phidaya alizungumza huku akimtazama mama Adrus aliye lewa chakari.

“Mimi ni mama mbaya”

“Mama mbaya kivipi jamani?”

“Mimi ni mama mbaya bwana”

Mama Adrus alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake jambo lililo pelekea Phidaya kuelewa ni kitu gani ambacho kinamsumbua mama Adrus.

“Basi twende ukapumzike”

“Hahaaa unataka nipumzike, nipumzike nina raha gani?”

“Najua, ila twende ukalale”

Phidaya akamshusha mama Adrus kwenye kiti hicho, taratibu akaanza kumkokota hadi katika chumba chake, akamlaza kitandani vizuri na kumfunika na blangeti kubwa kisha akamuwashia A/C kisha akatoka chumbani humo, akarudi jikoni na kuchukua vipande viwili vya mapaja ya kukua vilivyo kaangwa vizuri. Akamimina soda ya koka kola katika glasi kisha akavibeba na kuelekea chumbani kwa Cookie. Phidaya akagonga mlango wa chumba hicho mara tatu ila hakuweza kujibiwa chochote, taratibu akausukuma mlango huo na kuingia ndani, akamkuta Cookie akiwa amekaa kitako kitandani huku akiwa amejikunyata sana, na inaonyesha dhairi bado analia.

“Cookie”

“Mmmmm”

“Unasumbuliwa na nini mama yangu?”

“Hamana”

Cookie alizungumza huku akijifuta machozi yake usoni.

“Hapana una tatizo mdogo wangu, naomba unieleze nini kina kusumbua”

Phidya alizungumza hukua kimtazama Cookie usoni mwake.

“Ni Adrus ndio anaye kufanya ukose raha?”

Cookie akatingisha kichwa huku akimtazama Phidaya usoni mwake akimdhibitishia Phidaya kwamba alicho kizungumza kina ukweli ndani yake.

“Unataka nikufanyia nini ili uwe na furaha Cookie?”

“Nakuomba unisaidie kumrudisha Adrus mikononi mwako, tafadhali dada”

Cookie alizungumza huku akipiga magoti kitandani mwake. Phidaya akamtazama Cookie kwa muda kisha akamkumbatia kwa muda.

“Nimekuletea kuku basi ili uweze kuja kula kidogo”

“Sihitaji kula hadi nimuone Adrus hapa”

“Cookie jitahidi kidogo, toka asubuhi sijakuona ukiwa unakula chochote, tafadhali, ninakuomba uweze kula please”

“Siwezi namtaka Adrus wangu hapa”

Cookie alizungumza kwa msisitizo kiasi kwamba akamfanya Phidaya kuchoka katika juhudi za kumshawishi aweze kula. Phidaya akaitoa simu yake kwenye mfuko wa suruali yake aliyo ivaa, akaitafuta namba ya mume wake Eddy na kumpigia.

***

Eddy akaanza kujipapasa kwenye koti lake la suti na kutoa simu yake. Akaitazama kwa muda na kutambua kwamba ni Phidaya mke wake. Raisi Rahab akatupia jicho kwenye simu ya Eddy na kuona jina la Phidaya.

“Pokea tu simu usiwe na shaka juu yangu”

Rahab alizungumza kwa sauti ya unyonge na upole huku akimtazama usoni Eddy. Taratibu Eddy akapokea simu yake na kuiweka sikioni.

“Baby”

“Upo wapi mume wangu?”

“Kuna kazi ya kiserikali nina inafanya”

“Upo na Adrus?”

Eddy akaka kimya kidogo huku akimtazama Adrus anaye endesha gari hilo kwa mwendo wa kasi sana, akijitahidi kuhakikisha kwamba anafika mkoani Morogoro.

“Ndio”

“Nahitaji kuzungumza naye sasa hivi”

“Kuna nini kinacho endelea?”

“Wewe nipe tu nizungumze naye ni mazungumzo muhimu sana nahitaji kuzungumza naye”

“Tupo kazini mke wangu. Mungu bariki asubihi tutarudi hivyo nakuomba uwe na subra katika hayo mazungumzo”

“Sawa, ila jaribu kuzungumza naye kabla ya mimi kuzungumza naye. Kwa nini anamtesa mtoto wa watu, toka asubuhi huyu binti hajakula chochote anamtesa kwa nini?”

Phidaya alizungumza kwa uchungu mkubwa sana. Eddy hakuhona haja ya kuuliza ni nini alicho kifanya Adrus kwa maana anatambua kila kitu kilicho tokea asubuhi walipo kuwa wapo hospitalini.

“Tutazungumza asubihi mke wangu, sawa”

“Sawa mume wangu ila ninakuomba ukae naye, tusije kumpoteza binti wa watu”

“Usijali, nakupenda mama watoto”

“Nakupenda pia mume wangu, kazi njema”

“Asante, kuwa makini na watoto wote wawili”

“Sawa, Sa Yoo naye upo naye?”

“Hapana ila wataletwa nyumbani”

“Sawa”

Eddy akakata simu na kuruiweka katika mfuko wa suruali yake.

“Mkuu tunaingia Morogoro sasa”

Adrus alizungumza huku akipunguza mwendo kasi wa gari analo liendsha kwani mbele kuna matuta makubwa yanayo mfanya dereva yoyote anaye pita katika barabara hiyo kupunguza mwendo kasi wa gari lake anapo yakaribia.

“Piata njia ya kueleka Dodoma, kuna sehemu nitakuambia ukunje uelekee”

Raisi Rahab alizungumza kwa sauti ya upole na Adrus akafwata maelekezo hayo. Raisi Rahab akaenedea kumuelekeza Adrus hadi katika milima mikubwa.

“Simamisha gari hapo, huko tunapo kwenda hatuwezi kusonga mbele na gari”

“Sawa muheshimiwa”

Adrus akasimamisha gari kwenye eneo ambalo sio rahisi kwa mtu kuweza kuliona kwa haraka. Wakashuka wote watatu na wakaanza safari ya kuelekea mlimani zaidi ambapo ndipo dokta Wiliam. Ndani ya dakika kumi na tano, K2 na kikosi chake nao wakafika katika msitu huo, wakasmamisha magari yao katika eneo jengine kisha nao wakaanza safari ya kuelekea juu ya mlima huo ambapo ndipo alipo alipo elekea Rahab, Eddy na Adrsu.



“Ni pale”

Rahab alizungumza huku akionyesha kajumba kadogo sana kwa muonekano wake wa nje.

“Pale anaishi mtu kweli?”

Eddy aliuliza hukua akikishangaa kajumba hako.

“Ndio nyinyi twendeni”

Rahab alizungumza na wakazidi kusonga mbele, wakafika katika kijumba hicho. Rahab akaanza kugonga taratibu.

“Nani?”

Sauti ya dokta Wiliam ilisikika ikitokea ndani

“Mimi”

Mlango ukafunguliwa na wote watatu wakaingia.

“Karibuni sana”

Dokta Wiliam alizungumza hukua akiirudisha bastola yake nyuma ya kiuno chake na kuichomeka vizuri. Eneo kubwa la ndani ya nyumba hii imechongwa ndani ya mwamba mmoja mkubwa sana na kusababisha kwa ndani ionekane vizuri sana.

“Karibuni sebleni”

“Asante”

Dokta Wiliam akatangulia na kukaa kwenye sofa zilizopo katika eneo hilo, huku Rahab na Eddy nao wakikaa na kumuacha Adrus akiwa amesimama mita chache sana kutoka ilipo seble hiyo, huku akiendelea kuyachunguza mazingira ya ndani ya nyumba hii ya kisasa.

“Umezeeka daktari?”

“Sana na wewe umekua, ni muda mrefu sana hatujaonana, vipi wezako kina Fetty?”

“Wanaendelea vizuri, sasa hivi kila mtu ana maisha yake, wengine wapo ndani ya serikali yangu wengine wanaendelea kufanya biashara zao, kila mmoja ili mradi kwamba ana fanya maisha yake”

“Safi sana, mumetoka mbali sana”

“Ni kweli, dokta huyu anaitwa Eddy ni makamu wangu wa raisi pia ni mtoto wa marehemu raisi Godwin. Eddy huyu anaitwa dokta Benjamini ni mtu ambaye alinifundisha maisha”

“Nashukuru sana kukufahamu daktari?”

“Nashukuru pia, japo ninamfahamu sana huyu kijana, toka na yeye alipo kuwa mdogo, sema sikumfwatilia sana”

“Unanifahamu?”

“Yaa ninakufahamu, kipindi unasababisha matukio ya kugoma shuleni kwenu kule Arusha nilikuwepo kwenye moja ya hospitali ya serikali, tulikufwatilia fwatilia sana kipindi kile ila tuliishia njiani katika kukufwatilia”

“Ahaa……”

“Ehee, nimefanikiwa kufanya utafiti wangu wa ile hali yako na nimeweza kugundua dawa ambayo unaweza kuitumia na kuwaua wale virus?”

Dokta Wiliam alizungumza huku akinyanyuka na kueleka kwenye kabati lake la kuhifadhia dawa, jambo lililo mfanya Eddy kujawa na maswali mengi juu ya hao virus.

“Una virus gani?”

Kabla Rahab hajajibu kitu cha aina yoyote, mlango ukagongwa na kuwafanya wote kutazama mlangoni hususani Adrus aliye kaa karibu kabisa na mlango huo.

“Dokta ulitarajia mgeni yoyote usiku huu?”

Rahab alizungumza huku akisimama.

“Hapana”

Dokta Benjamini alizungumza huku akitetemeka, akatembea kwa haraka hadi kwenye computer zake mbili kubwa zilizopo mezani, akaweka upande wa kamera alizo zitega nje ya nyumba yake hiyo. Akaona kundi kubwa la watu wenye silaha wakiwa wamesimama mlangoni.

“Tumevamiwa”

Kauli ya dokta William ikamfanya kila mmoja kuchomoa bastola yake alipo ichomeka. Kwa haraka Rahab na Eddy wakamsogelea dokta William sehemu alipo simama na kuanza kutazama video hizo zinazo rekodiwa na kamera za ulinzi.

“Huyu si yule mwanamke mshenzi aliye ungana na wale magaidi?”

Eddy alizungumza huku akimuelekezea kidole K2.

“Ndio”

Rahab alijibu huku mapigo ya moyo yakianza kumuenda kasi

“Shiitiiii pumbavu sana”

“Huyu kijana kwa nini ameamua kuwaleta hapa?”

Dokta Wiliam aliendelea kuzungumza huku akimtazama kijana huyo anaye mfahamu ambye ndio mshauri wa John kaka yake K2.

“Mkuu”

Adrus alizungumza huku akiwafwata walipo simama

“Ndio”

“Inabidi tuondoke hapa, mzee kuna mlango gani wa kutokea mwengine hapa?”

“Hatuwezi kutoroka”

Eddy alizungumza na kumfanya kila mtu ndani ya hichi chumba kushangaa kwa maamuzi yake.

“Mbona hafungui, na kajumba kenyewe mbona kagodo sana?”

K2 aliuliza kwa dharua huku akiendelea kuitazama nyumba hii ya dokta William.

“Ni nyumba kubwa kwa ndani”

“Au mzee mwenyewe hayupo?”

“Huwa hana desturi ya kuondoka huku”

“Vunjeni mlango”

K2 alishauri.

“Sio ustarabu mzuri”

“Sasa tutaendelea kukaa hapa nje na kupigwa na baridi hadi muda gani?”

“Tuvute subra mdogo wangu”

John alizungumza kwa sauti ya upole iliyo jaa hekima ndani yake, kwa namna moja unaweza kuhisi ni mtu mwema ila kwa upande mwengine ni mtu aliye jaliwa kuwa na roho mbaya sana na hapo alipo ana uchu mkubwa sana wa madaraka ya kuiongoza nchi ya Tanzania.

“Eddy tunafanyaje jamani?”

Raisi Rahab alizungumza huku akiendelea kujawa na wasiwasi mwingi sana kiasi cha kumshangaza hadi dokta Wiliam kwani alisha mzoe Rahab kwamba ni mtu mwenye maamuzi magumu na ni jasiri sana asiye ogopa mapambano ya aina yoyote.

“Dokta nenda kawafungulie mlango”

“What……?”

“Ndio”

“Eddy acha kututania, dokta akafungue mlango, si tutakufa humu ndani”

Rahab aliuliza huku jasho likimshuruzika kwenye paji lake la uso.

“Tutajificha humu ndani na tutahitaji kuweza kusikia ni nini kilicho waleta huku kwa dokta”

Ukimya ukatawala kidogo huku wakitafakari nini cha kuzungumza. Dokta Wiliam kwa haraka akaanza kuongoza kwenye moja ya chumba huku kwa ishara akiwaita, wakamfwata kwa nyuma hadi ndani ya chumba hicho.

“Ingieni humu na mutulie, chochote kitakacho nipata ninawaomba musitoke.”

“Dokta naomba utueleze kile ambacho kimetuleta huku”

Eddy alizungumza huku akimtazama dokta Wiliam usoni mwake, dokta Wiliam akamtazama Rahab aliye jawa na wasiwasi mwingi sana.

“Ninakuja”

Dokta Wiliam akakimbilia hadi sebleni, akachukua kitabu kimoja cheupe alicho kiandika siri zinazo husiana na maisha ya Rahab na kurudi hadi ndani ya chumba hicho.

“Hichi kitabu Rahab kitunze sana, ndio kina kila siri ya maisha yako, kutoka na kila kitu ulicho nacho mwilini mwako. Sawa”

“Sawa daktari”

Dokta William akafunga mlango, akakimbilia hadi katika mlango wa kuingilia humo ndani kwake, akaanza kujifuta jasho lake usoni kwa kutumia shati lake alilo livaa, akashusha pumzi kisha akafungua mlango huo.

“Habari yako dokta”

“Salama karibuni”

Dokta Wiliam alizungumza huku akiwa amejikaza sana kuto kuonyesha wasiwasi wake mbele ya watu hao. K2, kaka yake na mshauri wa kaka yake wakaka kwenye sofa huku walinzi wake wakizagaa katika eneo la seble hiyo wakiimarisha ulinzi.

“Mbona saa hizi kijana kuna nini?”

“Samahani kwa kuja muda huu, ila ninakuomba ukae tuzungumze daktari kuna jambo muhimu ndio limetufanye sisi tuweze kuja hapa”

Dokta Wiliam akamtazama John kwa macho makali kisha akakaa.

“Dokta kuna jambo ulisha wahi kunigusia juu ya siri za raisi wa hivi Rahab, sasa nahitaji kuifahamu hiyo siri”

“Hilo ndio lililo kuleta hapa kijana?”

“Ndio dokta, huyu ni bosi wangu, anatarajia kugombania uraisi kwa awamu inayo kuja, hivyo basi anahitaji kufahamu juu ya siri hiyo ili aitumie kuingia madarakani”

“Una akili wewe, nina waomba muweze kutoka ndani ya nyumba yangu”

K2 akatabasamu huku akimtazama dokta Wiliam.

“Mimi huwa sipendi kupindisha pindisha kauli zangu. Jibu ni moja, utatuambia au hutuambii?”

K2 alizungumza huku akiikoki bastola yake na kuiweka tayari kwa mashambulizi.

“Siogopi kufa, miaka sabini na nne niliyo nayo imenitosha kabisa kuwepo duniani, fanya chochote unacho hitaji kukifanya”

K2 bila haya ya kujishauri mara mbili akampiga dokta Wiliam risasi ya paja lake na kumfanya dokta Wiliam kulia kwa uchungu mkali utikanao na maumivu makali sana.

“K2 nini unafanya?”

“Kaka tumekuja kwa jambo moja ya nini kubembelezana, unataka uraisi au hutaki?”

K2 alizungumza kwa ukali huku akimtazama kaka yake usoni. Swali hilo likamfanya kaka mtu kutulia kimya kwani anahitaji uraisi kwa njia yoyote.

“Eddy wanamuua dokta wa watu”

Rahab alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake. Eddy wakatazamana na Adrus, Eddy akatoka kutoka katika chumba hicho ila Adrus akamshika mkono na kutingisha kichwa chake.

“Tunahitaji kuijua siri hiyo haraka iwezekanavyo”

“Malaya wewe siwezi kukuambia kitu cha aina yoyote”

“Unasemaje wewe?”

“Kafir*****”

Tusi la Dokta Wiliam likamfanya K2 asimame kwa hasira sana, akamsogelea dokta Wiliam na kaunza kuminya koo lake kwa hasira sana.

“Unazungumza au huzungumzi?”

Dokta Wiliam akaendelea kukoroma. Galfa milio ya risasi ikaanza kusikika huku walinzi wo wakianguka mmoja baada ya mwengine. Shambulizi hilo linalo fanywa na Eddy akiambatana pamoja na Adrus, liamfanya K2 kumtumia dokta Wiliam kama ngao yake ya kuto kushambuliwa kwa risasi huku wakianza kutoka naye nje. Walinzi wengine wakawahi kumtoa muheshimiwa John ndani ya nyumba hiyo. Mshauri wake akajaribu na yeye kujikoa maisha yake ila akachelewa na kujikuta akipigwa risasi za miguu na kuanguka kabla hata hajaufikia mlango.

“Muangalie muheshimwia raisi”

Adrus alizungumza huku akizidi kuonga mbele akaindelea kuwashambulia watu wa K2 ambao baadhi wametoka nje ya nyumba hiyo huku wengine wakiwa ndio wamesha fariki kwa kupigwa risasi. Eddy akarudi katika chumba walicho kuwepo, akamkuta Rahab akiwa amekaa chini huku akilia kwa uchungu.

“Hei tuondoke”

“Eddy nitakufa leo”

“Huwezi kufa tupo kwa ajili yako”

“Naogopa”

“Usiogope”

Eddy alizungumza huku akimshika Rahab mkono na kumnyanyua, wakatoka ndani ya chumba hicho na kurudi sebleni. Wakamkuta kijana ambaye aliowaongoza K2 kuja katika eneo hilo akijiburuta akijaribu kutoka nje. Rahab kwa haraka akamfwata na kumvutia ndani.

“Unajua nini kuhusiana na mimi eheee?”

Kijana huyo akastuka sana kumuona raisi Rahab akiwepo katika eneo hilo.

“Nakuuliza unajua nini kuhusiana na mimi?”

“Ni….ni……buku”

“Nini zungumza kabla sijakumwaga ubongo wako”

Raisi Rahab alizungumza huku akiielekezea bastola yake katika kichwa cha kijana huyo.

“K2 na….na kaka yake wanataka ku….kuua ili…..ili wachukua madaraka wao”

Habari hiyo ikamstua sana Eddy, akamtazama kijana huyu kwa mcho makali, akakumbuka mashambulizi ambayo yalitokea siku kadhaa hapo nyuma. Akatoa simu yake mfukoni na kumpigia Adrus, simu ya Adrus ikaita kwa muda kisha ikapokelewa.

“Ndio mkuu”

“Hakikisha kwamba huyo mwanaharamu mwanamke, unatia mikononi mwako sawa”

“Sawa mkuu”

“Ikiwezekana hakikisha kwamba unamua hata huyo kaka yake, kwa maana wana nia mbaya na raisi Rahab”

“Sawa mkuu”

Eddy akakata simu na kumtazama kijana huyo aliye lala chini akiendelea kuugulia kwa maumivu makali. Eddy akampiga kijana huyo risasi mbili za kifuani na akafa hapo hapo.

“Mbona umemua?”

Rahab aliuliza huku macho yakiwa yamemtoka huku machozo yakiendelea kumwagika usoni mwake.

“Msaliti huwa hana nafasi kwenye maisha ya hapa duniani. Niambie ni siri gani hiyo wanayo taka kuitumia ili kukuua na kukutoa madarakani?”

Taratibu Rahab akanyanyuka, akamtazama Eddy huku akiendelea kulia, japo alitamani siri hiyo aweze kuidhibitisha dokta Wiliam, ila imshindika, inamlazimu aizungumze yeye mwenyewe.

“Najua hichi ninacho kwenda kikizungumza huto kiamini, ila ndio ukweli kuhusiana na mimi. Eddy mimi sio binadamu, Rahab alisha kufa miaka mingi sana ya nyuma ila nili…………”

Mlio wa risasi ulio sikika ukitokea kwa mmoja wa wafuasi wa K2 aliye amejeruhiwa, ukaikatisha sentensi ya Rahab na kumfanya atoe macho ikionyesha risasi hiyo kuna sehemu imeingia katika mwili wake jambo lililo mfanya Eddy kuchanganyikiwa sana.


Eddy kwa haraka akampiga risasi mlinzi huyo wa K2 aliye salia na kumua hapo hapo.

“Rahab, Rahab”

Eddy alita huku akimtingisha Rahab ambaya taratibu nguvu za mwili wake zimesha. Eddy akamshika Rahab mgongoni na kukuta akimwagikwa na damu, eneo ambalo ndipo risasi hiyo aliyo pigwa imeingia. Kwa haraka akambeba na kutoka naye ndani ya nyumba hii huku kitabu hicho akiwa amekichomeka kwenye koti lake la suti. Kwa umakini mkubwa sana kaana kushuka kilima hicho huku akijitahidi kuhakikisha kwamba haanguki. Kila jinsi anavyo zidi kwenda mbele ndivyo anavyo zidi kusika majibizano ya risasi.

K2 na watu wake wakazidi kuchannganyikiwa kwani mtu mmoja ambaye wnapambana naye unaweza kuhisi ni kundi la watu zaidi ya kumi kwani kila risasi wanavyo fyatuliwa ni lazima mpambe wao mmoja aweze kuanguka chini kwa kujeruhiwa au kupoteza maisha. K2 akafika kwenye gari alilo kuja nalo kwa haraka akamsukumia dokta Wiliam ndani ya gari huku kaka yake naye akiingia upande wa pili, akawasha gari na kuodoka eneo hilo kwa mwendo wa kasi na kuwaacha walinzi wanne wakijaribu kumzuia Adrus ambaye tayari kwao amekuwa ni mwiba wa kuotea mbali.

Walinzi hao hawakuwa kikwazo cha kumzuia Adrus, komandoo aliye pitia mafunzo ya ukomandoo na kupambana na magaidi wa kila aina na kufanikiwa kuwashinda. Ndani ya muda mfupia akawa tayari amesha walaza chini walinzi hao, akaingia kwenye moja ya gari na kuondoka kwa mwendo wa kasi kueleka kule walipo kwenda K2 na kaka yake.

Eddy akafika katika eneo ambalo waliliacha gari walio kuja nalo. Akafungua mlango wa siti ya nyuma akamlaza Rahab kiupande, kisha kwa haraka akaingia upandwe wa dereva, akawasha gari, akalirudisha nyuma kwa kasi akaliweka sawa na kuanza kuondoka katika msitu huo kwa mwendo wa kasi.

Milio ya risasi, iliweza kuwastua wanajeshi waliopo katika kambi iliyopo karibu kabisa na milima hiyo ya Ukaguru. Vikosi kadhaa vya wanajeshi wapatao thelethini wakiwa na bunduki pamoja na mbwa wakubwa wakanza kuzunguka milima hiyo kuhakikisha kwamba wale wote walio husika katika mashuambulizi hayo ya risasi walio kuwa wakiisikia hawatoki.

Eddy gafla akajikuta akifunga breki za gari analo liendesha. Roli kubwa la jeshi liilo beba wanajeshi kasha lilifunga barabara hiyo nyembamba ya kutoka katika msitu huo. Wanajeshi hao wenye silaha wakaanza kumuamrisha dereva wa gari hilo kutoka ndani ya gari hilo. Eddy akamtazama raisi Rahab aliye mlaza siti ya nyuma, kisha akafungua mlango wa gari hilo huku akinyoosha mikono yake juu. Wanajeshi hao kwa haraka wakamtambua kwamba ni makamu wa raisi ili kuhakikisha kwamba ni yeye wakamsogelea karibu.

“Muheshimiwa vipi?”

“Sio salama, nipo na muheshimiwa raisi siti ya nyuma anatakiwa kuapata matibabu ya haraka sana”

Eddy alizungumza kwa msisitizo na kumfunya mwanajeshi mmoja kuchungulia siti ya nyuma huku akimulika ndnai ya gari hilo kw akutumi tochi yenye mwanga mkali sana.

“Tumuwahishe kwenye hospitali yetu”

“Sawa fungueni njia, pika kuna kijana wangu mmoja anawafukuzia majambazi walio tuvamia, hakikisheni kwamba muna wafwatilia kwa umakini sana”

“Sawa muheshimiwa tumekuelewa”

Eddy akaingia ndani ya gari huku mwanajeshi mmoja mwenye taaluma ya udaktaria akaingia siti ya nyuma ili kuanza kumpa huduma ya kwanza raisi Rahab. Eddy akawasha gari na kuondoka eneo hilo huku mbele kukitangulia gari mbili za jeshi.

“Huyu mshenzi bado anatufukuzia?”

K2 alizungumza huku akitazama kioo cha pembeni yake na kuona moja ya gari lao jinsi linavyo wafwata kwa kasi sana.

“Una silaha hapo?”

“Kaka huwezi kupambana na huyo mshenzi, wewe tulia tu tushindane naye hapa baranani”

K2 alizungumza huku akizidi kuongeza mwendo kasi wa gari analo liendesha. Adrus naye katika umahiri wa uendeshaji wa magari yupo vizuri sana, kisha cha kuweza kuhimili kasi ya gari hilo na kukwepa kila kikwazo kinacho kuja mbele yake.

Gafla K2 akafunga breki za gafla huku akijitahiku kulikwepa roli moja aina ya Scania lililo sheheni mifuko ya smeti, linalo tokea mkoani Dar es Salaam, hapakuwakua na jinsi yoyote zaidi ya kulitoa gari hilo nje ya barabarani na kuanza kuivaa miti iliyo kando kando ya barabara hiyo. Taa za lori hili zikamcnaganya Adrus na kujikuta akifanya maamuzi magumu ya kulipindua gari lake na kulifanya lianza kuserereka barabarani, na dereva wa lori hilo akajitahidi kwa juhudi zake zote akahakikisha kwamba analikwepa gari hilo na kwa bahati nzuri akafanikiwa kulikwepa gari hilo ila kwa bahati mbaya nalo lori hilo nalo likaanguka na kuingia kwenye mtaro ulipo pembezoni mwa barabara hiyo. K2 akaanza kuwasha gari hilo lililo zama.

“Vipi?”

“Limezima”

“Jaribu kuliwasha”

“Nashindwa kaka”

K2 alizungumza huku akijitahidi kuwasha gari hilo, akashungulia nje na kushudia jinsi magari yalivyo pata ajali barabarani. K2 akashuka kwenye gari hilo akazunguka mbele ya gari hilo na kushuhudia jinsi gari hilo lilivyo potendeka pondeka kutokna na kugonga miti mingi sana.

“Shitiii…….”

“Vipi?”

John alizungumza huku akishuka kwenye gari hilo.

“Gari limepondeka sana sidhani kama linaweza kuwaka”

K2 alizungumza huku akifungua bonet ya gari hilo na kukuta kukiwa na moshi mwingi.

“Inabidi tutembee kwa miguu tunatua mbele ya safari itakavyo kuwa”

K2 alimshauri kaka yake

“Na huyu mzee ndani ya gari?”

“Tunaondoka naye?”

“Atatufia njiani bwana, tuachane naye tusije tukakamatwa”

“Kaka ila huyu anajua siri za Rahab?”

“Siri, siri za kazi gani bwana, tunatakiwa kuondoka katika eneo hili. Usalama wetu kwanza bwana”

K2 akaka kimywa kwa muda kisha akafungua boneti ya gari hilo, kisha akarudi upande wa dereva, akawasha gari hilo kwa bahati mbaya likaendelea kuto kuwaka. Hapakuwa na jinsi ya wao kuweza kufanya zaidi ya kuanza kutembea kuhakikisha kwamba wanakomboa maisha yao.

Adrus akastuka kutoka katika kupoteza fahamu kwani ajali hiyo kidogo ikamfanya kuzimia. Taratibu Adrus akafungua mkanda wa siti yake kisha taratibu akatoka ndani ya gari hilo, akasimama huku akiyumba yumba. Akatazama jinsi mgawanyiko wa magari ulivyo hapa barabarani, akaliona gari la kina K2 sehemu lilipo, taratibu akaanza ktembea huku akiyumba yumba, akapiga hatua kadhaa na kujikuta akianguka chini.

Akasimama tena na kuanza kutembea hadi lilipo gari la K2 akatoa bastola yake na kuchungulia ndani, akamuona dokta Wiliam akiwa amelala siti ya nyuma huku akiwa analalamika kutokana na jeraha la risasi aliyo pigwa.

“Dokta”

“Mmmmmm”

“Wapo wapi hawa washenzi?”

“Wamekimbia”

“Upo vizuri?”

“Hapana”

Adrus hakuwa na jinsi zaidi ya kufungua mlango na kumtoa dokta Wiliam. Adrus kwa haraka katoa simu yake mfukoni mwake akampigia Eddy.

“Vipi Adrus umewakamata?”

“Samahani muheshimiwa, sijafanikiwa kuweza kumpata, nimepata ajali”

“Eneo gani?”

“Silifahamu kwa haraka haraka ila nahisi bado sijatoka ndani ya mkoa wa Morogoro”

“Sawa si barabara ya kuelekea jijini Dar es Slaama?”

“Ndio muheshimiwa”

“Basi vikosi vya jeshi vinakuja hapo kukuchukua haraka iwezekanavyo, muheshimiwa raisi ameshambuliwa kwa risasi na hapa ndio tumefika katika hospitali ya jeshi”

“Ooohoo Mungu wangu vipi hali yake?”

“Hali yake sio nzuri, rudi hapa unisaidie katika hili”

“Je niwafwatilie hawa wavamizi?”

“Achana nao”

“Sawa muheshimiwa”

Adrus akakata simu, hazikupita hata dakika tano gari mbili za jeshi zikasimama barabarani wakashuka wanajeshi na kuanza kutawanyika katika eneo hilo huku wakiwa na bunduki mikononi mwao. Wakaoelekea katoka eneo lilipo gari la K2.

“Adrus”

“Ndio mimi”

“Okay tumeagizwa kuondoka nawe”

“Sawa sawa, nina mgonjwa hapa inatakiwa kusaidiwa”

Wanajeshi hao wakamnyanyua dokta Wiliam na kuondoka naye katika eneo hilo.

Madaktari wa jeshi wote wakabaki wakiwa wamejawa na mshangao mkubwa sana mara baada ya kumuona jereha la raisi Rahab likianza kujifunga taratibu tu mara baada ya kuitoa risasi hiyo.

“Dokta ni nini hichi?”

Nesi msaidia aliuliza huku akiwa amejawa na mshangao mkubwa sana kwani kwenye maisha yao hawajawahi kuona jerala la mgonjwa lijifunga lenyewe na kurudi katika hali ya kawaida. Kwa raka raisi Rahab akanyanyuka kitandani na kukaa kitako huku macho yakimtoka na yamejaa uwekundu ambao ukazidi kuwashangaza dakatari hawa wawili pamoja na nesi mmoja. Rahab akajitazama kifuani mwake ambapo maziwa yake yapo wazi. Akawatazama madaktari hawa na kwa haraka akamshika dokta mmoja na kumvunja shingo na kumua hapo hapo jambo lililo wafanya daktari mmoja na nesi wake kujawa na mshangao mkubwa ulio ambatana na woga mwingi sana.



Kurupushani ya daktari na nesi wake wanao jitahidi kuyaokoa maisha yao kutoka kwa raisi Rahab ambaye tayari amesha muuoa mwenzo mmoja, zikawafikia wanajeshi walio simama mlangoni pamoja na Eddy ambaye muda wote alikiwa akimuomba Mungu aweze kufanya muujiza wa kumsaidia raisi Rahab aweze kupona kwa maana hajui atawajibu nini Watanzania walio mpigia kuru na kumchagua kwa ushindi mzito sana. Wakaingia ndani ya chumba hicho cha upasuaji na kumkuta raisi Rahab akiwa amewanyanyua nesi na daktari kwa mikono yake miwili huku akiwa amewashika shingo zao na kuwaning’iniza hewani

Si Eddy wala wanajeshi hawa watatu alio kuwa nao waliwezea kuamini tukio hilo kwa haraka sana. Bumbuwazi zito lilio wakamata, likaja kupotea kwa kusikia vishindo vya nesi na daktari huyo kuangushwa chini huku wakiwa tayari wamesha poteza maisha yao. Kitendo cha Rahab kuwageukia na kuwatazama kwa macho yanayo tisha, kikawafanya wanajeshi hao watatu kutupa bunduki zao na kuondoa eneo hilo kwa kukimbia na kumuacha Eddy akiwa anatetemeka mwili mzima kwani anaye muona hapa si yule Rahab aliye zoea kumtomasa tomasa kitandani, bali ni jini linalo tisha sana.

***

K2 na kaka yake wakatembea kwa umbali wa kama kilomita moja na nusu, wakakuta gari aina ya Fuso likiwa limesimamisha pembezoni mwa barabara huku vijana wake wakiwa anashuhulika na utengenezaji wa tairi lililo pasuka.

“Niaje Chalii zangu”

Kaka yake K2 alianza kuzungumza kwa lafudhi ya kichaga na kuwafanya vijana wawili walio simama nyuma ya gari hilo kukaa kimya kwa muda huku wakiwatazama.

“Safi niaje broo”

“Ni shega machalii zangu, nini tatizo hapa”

“Ahaa…….tairi lime kuny***”

Alijibu kijana mmoja huku akitazama wezake wengine watatu wanao shuhulika na tairi la mbele la gari hilo.

“Aisee poleni sana”

“Asante, vipi mbona usiku huu peke yenu munatembea tembea kwema?”

“Kwema machalii zangu, hapo chini fulani tumepata ajali kwa bahati mbaya gari haijawaka, tusonge mbele ili tupate msaada wa hapa na pale si unajua kukaa poridi na nipo na shem wenu hapa raisi wanaweza kuletea ujinga”

K2 akamtazama kaka yake kwa mshangao baada ya kumtambulisha kwamba yeye ni mwanamke wake na si demu wake.

“Aiiisee poleni sana, munakwenda wapi?”

“Dar es Slaaam”

“Ohoo sisi wenyewe tunakwenda huko huko, ngoja wanamalizia kufunga hiyo tairi hapo”

“Ahaa shukrani sana”

“Aisee hamjamaliza hiyo tairi kuifunga?”

“Ndio tunamalizia bolti ya mwisho mkuu”

“Poa poa”

“Manzi wako anaitwa nani?”

“Ahaaa anaitwa Maria”

“Ohoo una Manzi mzuri, shemela pole kwa ajali bwana, si unajua barabarani humu mambo mengi”

“Kweli, asanteni jamani”

K2 alizungumza kwa sauti alini na iliyo jaa mapozi kiasi cha kumfanya kaka yake naye kushangaa. Baada ya dakika kama tano wakajumuika na vijana wawili kupanda nyuma ya fuso hiyo iliyo funikwa na turubai.

“Haya ni magunia ya nini?”

John aliuliza huku akimtazama mmoja wa kijana.

“Ni magunia ya viazi na mchele”

“Ahaa hivi hii biashara inalipa kweli?”

John alijifanya kuuliza uliza ili mradi kuendelea kuwapumbaza vijana hawa wasiweze kuwafikiria wala kuwa na mashaka na wao.

“Yaa inalipa, ukiwa na gari lako kama hivi na una shamba lako, basi biashara inakwenda vizuri kishenzi”

“Ohoo labda ni kama mtaji wa bei ngapi hivi unaweza kusaidia hii biashara ikaweza kuleta faida”

“Kama unaingia shamba hivi, ukiwa na milioni zako kumi, unapata shamba zako za maana na unatoa mzigo wa kufa mtu”

“Ohoo sawa sawa”

“Shem mbona upo kimya?”

“Hamana nawasikiliza?”

“Baby hujaumia hivi?”

John alizungumza huku akimtazama K2 na kumshika shika kiuno chake. K2 akatingisha kichwa akimaanisha kwamba hajaumia sehemu yoyote.

‘Bwana unanipandisha nyege’

K2 alimnong’oneza kaka yake na kumfanya aitoe mikono yake hiyo kwa maana huyo ni mdogo wake wa kike wa tumbo moja japo baba ni tofauti. Gafla gari likasimamisha na kuwafanya K2 na kaka yake kupata mashaka.

“Shukeni chini”

Zilisikika sauti za kiume zikizungumza kwa ukali sana. K2 akataka kichomoa bastola yake nyuma ya kiuno chake ila kaka yake akawahi kumshika mkono wake kwa maana vijana hawa wanaonekana kuto kuwa na waswasi wa aina yoyote.

“Ni kina nani hao?”

John aliuliza huku akimtazama kijana mmoja.

“Ni askari, yaani hawa jamaa kwenye hii beria ya hapa huwa wanatuzingua sana, hawapatani nana na bosi wetu”

“Ahaaa”

“Wamesha washusha bosi, utingo na dereva, ngoja watakuja huku na mitochi tochi yao”

K2 akamtazama kaka yake huku akishusha pumzi nzito.

“Oya funua turubai”

Kijana mmoja aliye kaa karibu kabisa na sehemu ya kushukia, akafungua turubai hilo, askari wawili walio shika tochi zenye mwanga mkali sana, wakaanza kumulika ndani ya gari hilo.

“Oya na nyinyi shukeni”

Askari mmoja alizungumza na kumfanya K2 kuichomo bastola yake na kuichomeka chini ya gunia moja la viazi pasipo mtu yoyote kuweza kuona tukio hilo, taratibu wakaanza kushuka mmoja baada ya mwengine.

K2 akawa wa mwisho kushuka kwenye gari hilo huku akiwatazama askari hawa kwa umakini mkubwa sana.

“Oya nyinyi mafala mumeanza lini kupakiza abiria eheee?”

Askari mmoja alizungumza huku akiwafwata bosi wa gari hilo na dereva wake amabao wamesimama kando ya barabara wakizungumza na askari wengine walio wazunguka huku wakiwa wameshika bunduki zao.

“Wameomba msaada bwana vipi wewe?”

Mmiliki wa gari hilo alizungumza huku akifoka sana inaonyesha tayari alisha tibuliwa.

“Hawa wakivaa vinguo vyao vya kaki basi wanaringa kishenzi”

K2 alizungumza kwa sauti ya chini na kumfanya askari aliye simama karibu yao kumtazama.

“Unasemaje wewe?”

“Sijasema kitu”

“Zungumza ulicho kisema”

Askari huyo alizungumza huku akimfwata K2 kwa jazba jambo lililo mfanya John kuwahi kumshika polisi hiyo kifuani kwa lengo zuri la kumzui. Askari huyo akautoa mkono wa John kwa nguvu sana.

“Unanishi, unishika wewe mjinga”

Askari huyo alizungumza kwa kufoka na kuwafanya askari wengine kugeikia eneo hilo na kuangali mzozo huo mpya.

“Huwezi kumshika demu wangu”

“Demu wako ndio azungumze upuuzi juu yetu eheee?”

“Amezungumza nini huyo?”

Askari mwengine akadakia kesi hiyo huku akisogelea eneo hio huku bundiki yake akiwa ameishika vizuri

“Huyu chiki anasema sisi eti ohoo tunajisikia tukivaa gwanda zetu”

“Kwanza wachuchumae, wanazungumzaje wakiwa wamesimama”

“Samahani kaka zangu kama nimewaudhi ninawaomba munisamehe jamani”

K2 alizungumza kwa sauti ya upole iliyo wafanya askari hao kumkodolea macho.

“Huyu fala anajidai kunishika shika kifuani mwangu, unajua ni nimeihangaikia vipi hii nguo kule Moshi?”

Askari huyo alizungumza kwa hasira huku akimtazama John usoni mwake.

“Jamaa mbona unasifa sana, hiyo jezi yako si kama tambara la deki tu”

Maneno hayo ya John yakawa kama yameibua hasira kali ya askari hao, kwani kila mmoja akaanza kumshambulia kwa mateke. Kitendo hicho kikamnyima K2 uvumilivu, kwani kaka yake hawezi kupigwa mbele yake, kwa haraka akampiga teke la shingo askari kiherehere aliye sababisha mambo kufikia hapo. Teke hilo likamuangusha chini askari huyo na kumfanya apote fahamu hapo hapo kwani toka kuzaliwa kwake hakuwahi kukutana na teke zito kama hilo.

***

Gafla Phidya akastuka kutoka usingizini huku akihema sana, kwa haraka akawasha taa ya pembeni mwa kitanda chake kisha, akachukua night dreas yake na kuivaa vizuri, kwa haraka akatoka chumbani kwake na kuelekea katika chumba cha watoto wao na kuwakuta wakiwa wamelala fofo. Akashusha pumzi nyingi sana, kwani ndoto aliyo iota ni mbaya sana kiashi cha kwamba imempa wasiwasi mwingi sana, kwa haraka akarudi chumbani kwake na kukumbuka kwamba mtu ambaye hayupo karibu na nyumbani kwake ni Eddy mumewe. Akaichukua simu yake na kumpigia Eddy. Simu ya Eddy ikaanza kuita ila haikupokelewa, akarudia tena kuipiha ila ikaita pasipo kupokewa kabisa, jambo lililo zidi kumpa wasiwasi mwingi na mashaka.



“Poke poke simu mume wangu”

Phidaya alizungumza huku mikono ikimtetemeka sana. Akarufia tena kupiga simu ya Eddy ila matoke yakawa ni yale yale ya kuto kupokelewa. Phidaya akatoka tane chumbani kwake na kuelekea katika chumba cha Cookie, akaanza kugonga, baada ya muda kidogo mlango ukafunguliwa

“Dada vipi?”

“Una..una namba ya Adrus anayo itumia hivi sasa?”

“Ndio”

“Naomba unitajie kama unaifahamu”

Cookie akaanza kumtajia Phidaya namba ya Adrus, kisha Phidaya bila ya kusema asante akaanza kuondoka na kumfanya Cookie ashangazwe na tukio hilo la kugongewa mlango usiku wa manane. Phidaya akaingia chumbani kwake huku simu hiyo akiwa ameiweka sikioni mwake. Simu ikaanza kuita hadi ikakata jambo lililo mfanya mapigo ya moyo kumuenda kasi hadi jasho jingi likaanza kumwagika usoni mwake. Akapiga tena simu ikapokelewa

***

Adrus akaitoa simu yake mfukoni kwa bahati mbaya akawa emechelewa kuipokea. Kabla hajachukua maamuzi ya kuipiga namba hii mpya inyo mpigia, simu yake ikaanza kuita kwa namba hiyo hiyo. Akamtazama dokta Wiliam aliye kaa siti ya pembeni yake huku akiendelea kuugulia jeraha la risasi alilo pigwa.

“Halooo”

Adrus aliwahi kuzungumza huku akimini kwamba mtu ambaye anaweza kumpigia kwa muda huu ni Naomi aliye muacha hotelini.

“Adrus”

“Ndio”

Adrus aliisikia sauti hii na kuanza kuifananisha huku akijitahidi kukumbuka ameisikia wapi.

“Upo karibu na mume wangu”

Swali hilo likamfanya Adrus aweze kumjua kwamba anaye zunumza naye ni mke wa makamu wa raisi.

“Ahaa….kuna sehemu yupo ila unaweza kuzungumza naye baadae kidogo”

“Ni wapi huko?”

“Ni maswala ya kikazi madam”

Adrus alijikuta akimuongopea Phidaya.

“Akitoka huko muambie kwamba nahitaji kuzungumza naye”

“Sawa madam”

“Ila yupo salama lakini?”

“Yaa yupo salama”

“Ohoo asante Mungu, haya baadae”

“Sawa madam”

Adrus akakata simu, wakafika katika geti kubwa la kuingilia katika kambi ya jeshi. King’ora cha hatari jeshini hapo kikaanza kusikika jambo lililo sababisha Adrus na wanajeshi alio kuwa nao ndani ya gari hilo kujawa na mshangao kwani king’ora kama hicho kipigwa basi ujue kambi ipo katika uvamizi.

“Rahab, Rahab”

Eddy alijitaidi kumuita Rahab ambaye bado anamtazama. Wanajeshi wengine wakaanza kukusanyika kwa kasi katika eneo la chumba hicho cha upasuaji huku wakiwa na silaha, hii yote ni kutokana na kupewa habari na wezao juu ya hali ya raisi wao. Rahab kwa kasi ya ajabu akaanza kuwashambulia wanajeshi hao kwa kuwavunja shingo zao. Kasi kubwa anayo itumia Rahab inawafanya wanajeshi hao kushindwa kufahamu ni jinsi gani ya kumzuia.

“Musimpige risasi”

Eddy alizungumza kwa nguvu mara baada ya wanajeshi kadhaa kushindwa kuvumilia.

“Rahab naomba unisikilize”

Eddy alizungumza kwa sauti ya upole huku kuzuia Rahab kuto kufanya chochote. Kwa kasi Rahab akamkamata Eddy shingo yake na kuanza kuiminya huku akimnyanyua juu taratibu. Wanajeshi uvumilivu ukawashinda na kuanza kumfyatulia raisi Rahab risasi ambazo hazikuzaa matunda ya kumdhuru mwili wake, kwani alicho kufanya ni kumtupa Eddy pembeni na kuwashambulia wanajeshi hao kwa kuwapiga huku wengine akiwavunja vuja viongo vyao vya mwili.

“Kuna nini kinacho endelea?”

Adrus aliuliza mara baada ya kushuka kwenye gari hilo walilo jia katika kambi hiyo ya jeshi.

“Ni raisi”

“Raisi amefariki?”

Adrus aliuliza huku akiwa amejawa na awasiwasi mwingi sana kwani aliambia kwamba raisi amepigwa risasi.

“Hapana raisi anawauma wanajeshi”

Kauli hiyo ya mmoja wa wanajeshi ikamstua sana dokta Wiliam, kwani yale mabadiliko ya Rahab aliyo kuwa akiyatambua kwamba yanaweza kutoka katika za hapa karibuni ndio haya aliyo yasiki.

“Anaua watu?”

Adrus aliendelea kuuliza kwa mshangao mkubwa sana.

“Ndio”

“Naomba unishushe kwenye gari”

“Dokta umemumia?”

“Hapana nishushe la sivyo kambi nzima hii itauwawa”

Dokta Wiliam alizungumza kwa msisitizo, kiasi cha kumfanya Adrus kuazidi kushangaa. Adrus akamshusha dokta William kwenye gari na wakaanza kueekea eneo la hospitali huku wakimsaidia dokta William kutembea kwa kasi kwani wanahitaji kuwahi kufika katika eneo la tukio.

“Dokta hembu niambe ni kitu gani ambacho kinaendelea?”

“Raisi wenu sio mtu wa kawaida?”

“Sio mtu wa kawaida kivipi?”

“Utaona”

Kabla hata hawajafika eneo la hospitali wakakutana na wanajeshi wakikimbia kila mmoja akijitahidi kuyaokoa maisha yake.

“Vipi?”

Mwajeshi aliye ungana na Adrus katika kumsaidia dokta William kufika katika eneo hilo la hospitali ya kijeshi aliwauliza wezake ambao wanakimbia.

“Musiende huko”

Mwanjeshi mmojaa lijibu bila ya maelezo ya kutosha na kuendelea kukimbia eneo ambao litakuwa ni salama.

“Twendeni”

Dokta William alizungumza huku akisonga mbele. Mwanajeshi huyo mara baada ya kuona wezake wanakimbia akaona hakuna haja ya yeye kwenda kujishihudia mauaji hayo yanayo semekana kwamba yanafanywa na raisi Rahab.

“Mbona unaondoka”

“Sihitaji kufa mimi”

Mwajeshi huyo alizungumza huku akimuachia dokta Willim mkono wake na kujumuika na wezake katika kukimbia.

“Twende”

Dokta William alizidi kuzungumza kwa kujiamini na kumfanya Adrus naye ajiamini huku moyoni mwake akiwa na shauku ya kuhitaji kuona ni nini kinahco endelea. Wakafika kwenye kordo ya kueleka katika chumba cha upasuaji na kukuta maili ya wanajeshi kama thelathini na nane ikiwa imelala chini. Mwili mmoja Adrus aliweza kuufahamu kwamba ni wa makamu wa raisi.

“Muheshimiwa, muheshimiwa”

Adrus alizungumza huku akimuachia dokta William na kumkimbilia Eddy sehemu alipo simama. Kwa bahati nzuri akamkuta Eddy akijinyanyua huku akihema sana.

“Muheshimi upo salama?”

“Mmmm…..Rahab. Rahab……”

Eddy alizungumza huku akihema sana kana kwamba ni mtu punyuka katika kifo. Taratibu Adrus akamsaidia Eddy kunyuka, akatazama eneo ambalo alimuacha dokta Wiliilm akiwa amesimama, ila hakuwepo.

“Doktaaaaa”

Adrus aliita kwa sauti ya juu sana ila hapakuwa na muitikio wa aina yoyote.

“Muheshimiwa unatakiwa kundoka eneo hili”

Mkuu wa kambi alizungumza hukua kiwa amefika katika eneo hilo akiwa na wanajeshi wake wawili.

“Hapana, Rahab ameelekea wapi?”

Eddy alijiuliza hukua kijiweka sana.

“Sifahamu”

Mtafuteni, hakikisha kwamba kambi nzima inafunga na hatoki nje ya kambi hii asije akelekea mtaani na kusababisha matatizo sawa”

“Sawa muheshimiwa”

“Adrus saidiana nami kumtafuta Rahab”

“Sawa muheshimiwa, ila dokta amepotea?”

“Dokta gani?”

“William”

“Eheee msakeni huyo naye. Panga vikosi vyako mzee”

“Sawa muheshimiwa”

Eddy kwa haraka akachomoa kitabu alicho pewa na dokta Willima kinacho onyesha siri za raisi Rahab. Akafungua ukurusa wa kwanza na kuanza kusoma maelezo yatokanano ya tatizo alilo nalo raisi Rahab. Katika kitu ambacho hakitakiwa kutumia Rahab anapo kuwa katika hali hiyo moja wapi ni risasi.

“Mzee hakikisha kwamba hapigwi risasi”

“Kwa nini muheshimiwa?”

“Ndivyo jinsi mutakavyo mpadisha hasira na zimeni hicho king’ora kwa maana hapendi kelele?”

Eddy alizungumza huku akiwa anasoma maelezo yaliyo andika katika kitabu hicho.

“Sawa muheshimiwa

“Adrus ongozana nami”

Eddy mara baada ya kumaliza kuzungumza mazungumzo hayo kwa haraka wakaondoka katika eneo hilo na kuanza kumsaka riasi Rahab ni wapi alipo. Dokta Wiliam akaanza kuchanganya chemical anazo zifahamu kwamba akizitumia hizo basi anaweza kuituliza hali ya Rahab ambayo ni hatari sana. Gafla Rahab akaingia ndani ya maabara hiyo alipo dokta Wiliam na kumkuta akiwa anaendelea kuchanganya chemical hizo.

“Unahisi unaweza kunizuia dokta”

Rahab alizungumza kwa sauti ya ukali sana ambayo inaumiza masikio ya mtu aliyuopo karibu yake na kama kuna chombo aina ya glasi, kikapasuka vipande vipande.

***

K2 na kusaidia na kaka yake wakawapa kipigo kikali askari hao, kisha wakaawaamrisha dereva na vijana akiwemo mmiliki wa gari hilo la mizigo kuingia ndani ya gari na kuondoka kwa kasi sana na kuwaacha askari hao wakiugulia maumivu makali sana waliyo yapata.

“Nyinyi ni kina nani?”

Kijana mmoja aliuliza huku akiwa amejawa na wasiwasi mwingi sana. K2 hajibu swali hilo zaidi ya kuichomoa bastola yake aliyo kuwa ameichomeka kwenye magunia hayo yaliyomo ndani ya gari hilo na kuwazidi kuwafanya vijana hao kuwaogopa.

“Sisi ni watu wema tu, ila askari walihitaji kutuchelewesha”

John kaka wa K2 alizungumza kwa sauti ya upole sana huku akimtazama kijana aliye uliza swali hilo. K2 akaichomea bastola yake kiunoni na kujilaza vizuri kwenye moja ya gania. Safari yao ikazidi kusonga mbele kwa usalama na hawakukutana na kikwazo cha aina yoyote hadi wanafika jijini Dar es Salaam. Wakashuka eneo la Ubongo maji yakiwa ni majira ya saa kumi na moja alafajiri, wakakodi taksi iliyo wapeleka moja kwa moja hadi katika jumba la bwana John, wakamlipa dereva huyo na kutulia ndani humo.

“Tumeenda bure na tumerudi na hasara”

K2 alizungumza kwa sauti ya upole.

“Laiti kama tungejua kwamba makamu wa raisi yupo ndani ya ile nyumba tungemuangamiza mule mule ndani”

“Tatizo lako wewe kaka una roho ya kike, umekaa kiuruma huruma sana, unajua kwamba unanikera muda mwengine”

K2 alizidi kuzungumza kwa ukali sana.

“Mimi leo nimefanya nini hadi unitupie mimi lawama hizo?”

“Hujui, una kera, laiti kama tungefanya shambulizi mapema sana, tungewakuta wamekaa sebeni. Ila kwa huruma zako ukajifanya tusubiri…Ohooo nisifunge mlango mara hooo vimepanda vimeshuka, yaani ungejua jinsi ulivyo nikera wala usinge zungumza.”

“Ila K2 mambo mengine sio ya kukurupuka?”

“Fala wewe kukurupuka nini sasa, wapo wapi vijana tulio kwenda nao. Wote si wamekufa kwa ajili yako wewe. Unataka uraisi unakuwa na roho ya kipuuzi jikaze mwanaume wewe. Siku nyingine tukipanga kufanya jambo la hatari kama hili, ukiwa na maamuzi ya kidada dada, nitakuacha ufanye mwenywe uone kama utakuja kuwa raisi”

K2 aliendelea kufoka na bwana John akanyamaza kimya kwani anamfaahamu K2 vizuri, ni mkorofi sana toka alipo kuwa mtoto mdogo sana na siku zote kwenye maisha yake huwa hakubali kushindwa na jambo lake alilo panga kulifanya na hadi mwiso wa siku yeye ndio anahitaji kuwa mshindi wa kila jambo liwe baya au zuri.

“Ni lini tunafanya mpango mwengine na safari hii nitamua mimi mwenyewe Rahab”

Bwana John alizungumza na kumfanya K2 kumpandisha na kumshusha kwa macho yaliyo jaa dharau, kisha akasimama kwenye sofa aliko kuwa emakalia. Akaanza kumfwata kaka yake sehemu alipo akamshika shati lake sehemu ya kifuani na kumvuta karibu yake huku akiwa amekazia macho, kisha akaanza kumnyona lipsi kaka yake jambo lililo mshangaza bwana John kwani huyu ni ndugu wa tumbo moja kabisa.



“K2 unafanyaje?”

Johna alizungumza huku akijitoa mikononi mwa K2.

“Nini maana ya kuniita mimi ni mpenzi wako?”

“Kumbuka kwamba sisi ni ndugu wa tumbo moja?”

“Ila si damu moja”

“Sawa ila pia kumbuka kwamba nina mpenzi”

“Kwa hiyo?”

K2 akamsukuma kaka yake na kumkalisha kwenye sofa, kisha kwa haraka akapanda juu ya mapaja yake na kumkalia. Akaanza kufungua vifungo vya shati la kaka yake.

“K2 hichi tunacho kifanya hakimpendezi Mungu mdogo wangu?”

“Tuliyo yafanya leo yanampendeza Mungu…..Mmmmm?”

K2 alizungumza huku na yeye akivua tisheti aliyo ivaa na kubakiwa na siriria, akaivua sidiria yake na kuuchukua mkono wa kulia wa kaka yake na kumshikisha ziwa lake.

“Nahitaji unikate kiu yangu hasira yagu ndio itaniishia”

K2 alizungumza huku akiendelea kuushikisha mkono wa kake yake katika ziwa lake la upande wa kushoto huku akiliminya minya kwa nguvu.

***

Dokta William akaanza kutetemeka mwili mzima huku akimtazama raisi Rahab ambaye anamsogelea taratibu huku mishipa yake ya damu ikiwa inaonekana vizuri sana kwenye mikono yake.

“Rahab tafadhali nakuomba utulie”

“Unahisi utanizuiaaaa”

Raisi Rahab alirudia sentensi yake kwa sauti ya ukali. Eddy na Adrus wakaisikia sauti hiyo sehemu inapo tokea na kwa haraka wakaanza kukimbilia katika eneo hilo la maabara. Adrus akawa wa kwanza kuingia huku akiwa ameishika bastola yake mkononi.

“Adrus usimshambulie”

Dokta William alizungumza kwa sauti ya juu na kumfanya Rahab kugeuka nyuma na kumtazama Adrus kwa macho makali hadi Adrus mwenyewe akaanza kutetemeka. Eddy akaingia na kusimama mbele ya Rahab huku akimtazama kwa kujiamini.

“Rahab naomba utulie”

Eddy alizungumza huku akiwa amekishika kitabu alicho pewa na dokta William masaa machache yaliyo pita. Dokta William akachukua moja ya bomba la sindano lililomo ndani ya hospitali hii, akavuta kiasi cha kemikali alizo zichanganya anazo amini ni dawa ambayo inaweza kutuliza hali ya hasiria ya na mauaji ya Rahab aliyo nayo kwa sasa.

“Rahabu kumbuka mimi na wewe ni wapi tulipo toka. Kumbuka furaha na michezo yote tuliyo cheza kitandani, kwa nini unahitaji kufanya mauaji mpenzi wangu”

Eddy alizungumza kwa sauti ya chini sana na kumfanya Rahab azidi kumsogelea kwa hatua za taatibu huku macho yake yakianza kutoa machozi ya damu jambo lililo washangaza Eddy na Adrus.

“Rahab nakupenda mpenzi wangu, nakuhitaji mpenzi wagu kwa nini unakuwa hivi?”

Eddy alizungumza huku wasiwasi ukizidi kumtawala moyoni mwake. Dokta William akaanza kunyata kwa taratibu, akafanikiwa kukaribia na kumchoma Rahab sindano hiyo ya mgongo na kuisukuma dawa hiyo kwa nguvu kabla hata hajaimaliza Rahab akageuka kwa kasi na kumsukuma kwa nguvu na kuangukia pembeni. Dawa hiyo ikaanza kufanya kazi kwa kasi mwilini mwa Rahab na baada ya sekunde kama arobaini na tano hivi taratibu akaanza kulegea na kuanguka chini na kupoteza fahamu. Kwa haraka Adrus akamkimbilia dokta Wiliam aliye angukia angukia mbali kidogo.

“Dokta, Dokta”

“Mmmmm”

“Vipi umeumia?”

“Mguuu, mguuu”

Kwa haraka Adrus akaanza kumpa huduma ya kwanza dokta Wiliam huku Eddy akiendelea kumchunguza raisi Rahab aliye alala chini. Wanajeshi wanne wakaingia katika maabara hiyo wa kiwa na bunduki, walipo mkuta raisi Rahab yupo chini, wakatoa ripoti kwa mkuu wao na baada ya muda kidogo mkuu wao akafikia akiwa na kikosi cha wanajeshi wengine.

“Mkuu imekuaje?”

“Mtafutieni chumba kitupo cha kuaminika tuweze kumuweka”

“Sawa muheshimiwa”

Eddy taratibu akasimama huku aki akimtazama Rahab aliye lala chini. Dokta William naye akanyanyuliwa na kutolewa katika chumba hichi na kupelekwa katika chumba cha matibabu.

“Naomba munipatie taarifa ya madhara yaliyo weza kutokana na jambo hili alilo lifanya raisi”

“Sawa muheshimiwa”

“Na kitu kingine hakikisheni kwamba hii taarifa haitoki nje ya hii kambi na kuwafikia waandishi wa habari”

Eddy alizungumza kwa msisitizo mbele ya wanajeshi hao. Kisha Raisi Rahab akatolewa katika chumba hichi cha maabara na kuhifadhiwa katika chumba kidogo kiasi kilicho tengenezwa madirisha ya nondo pamoja na mlango wa chuma kizito.

“Itisha kikao cha wakuu wote wa kijeshi katika kambi zote Tanzania”

“Sawa muheshimiwa”

Mkuu wa kambi hiyo akaondoka na kumuacha Eddy akiwa amesimama na Adrus ambaye hadi sasa hivi anajionea kama ni maigizo kwani raisi ambaye siku zote anamtambua kumbe ni kiumbe cha ajabu sana.

“Muheshimiwa”

“Naam”

“Inabidi sasa uweze kufanya maamuzi magumu”

“Kivipi Adrus?”

“Unatakiwa kuhakikisha kwamba unaichukua nchi na kwa mtazamo wangu sidhani kama raisi Rahab ana uwezo wa kuendelea kuiongoza hii nchi”

“Nitakaimu tu kama cheo changu ila siwezi kuwa raisi wa nchi”

“Muheshimiwa hapa hakuna kukaimu. Unatakiwa kuwa raisi”

“Nitawambia nini Watanzania?”

“Yapo mengi ya kuwaambia ikiwemo hali ya raisi aliyopo madarakani”

Adrus aliendelea kuzungumza kwa msisitizo mkubwa sana. Eddy akafumba macho yake huku akitazama jisni glas nyingi zilivyo pasuka pasuka ndani ya chumba hichi cha maabara.

“Ngoja tuangalie”

“Hakuna cha kuangalia muheshimiwa kwa kipindi hichi kilicho baki cha madaraka, ni lazima ukiongoze wewe, hii ni skendo mbaya sana endapo itatoka kwa raisi na kumbuka kwamba hii nchi uliipigania na kumpindua baba yako mzee Godwin, ni wakati wako sasa wa kufuta makosa yote ambayo aliyafanya baba yako. Ni wakati wa kuifanya Tanzania isimame tena, imetetereka katika uongozi wa huyu mama, ameshindwa kuhimili mikiki mikiki ya hata vijambazi vidogo vinavyo tumia AK47.

“Nimekuelewa Adrus”

Mkuu wa kambi hii ya jeshi iliyopo katika mkoa wa Morogoro, akamfwata makamu wa raisi na kumueleza kwamba wakuu wote wamesha kusanyika na wanamsubiria. Wakaondoka wote watatu na kuingia katika ukumbi mkubwa wa jeshi ulipo chini ya ardhi ambapo kuna Tv kubwa inayo karibia kujaa moja ya ukuta wa ukumbi huo. Picha ndogo ndogo za video zinazo waonyesha wakuu wa majeshi kutoka katika meneo mbali ya nchi ya Tanzania wamekusanyika na kwa kupitia njia hiyo wanaweza kufanya kikao na kika eleweka vizuri sana.

“Waziri wa ulinzi na usalama hayupo hapa?”

“Ngona niwasiliane naye”

“Pia wasiliana na waziri mkuu”

“Sawa muheshimiwa”

Mkuu wa kambi hiyo akafanya mawasiliano hayo huku akiendelea kutafakari nini anacho weza kukizungumza kwa wakati huu.

“Baada ya dakika tano watakuwa kwenye chanel”

“Sawa, ile ripoti mumesha niandalia?”

“Ndio muheshimiwa”

“Si kuna kamera za ulinzi zilizo weza kunasa matukio hayo?”

“Ndio”

“Niandalieni na ninahitaji muniletee vikiwa ndani ya laptop nahitaji kumuonyesha kila mmoja hapa”

“Sawa muheshimiwa”

Baada ya maagizo yote aliyo yatoa Eddy Godwin makamu wa raisi wa nchi ya Tanzania, kukamilika kutekelezwa ikiwemo waziri mkuu na waziri wa ulinzi na usalama kujumuika katika kikao hicho cha dharura, kikao kikaanza rasmi.

“Naamini kwamba wengi wenu mutashangazwa kwa hili lililo tokea, ila jinsi utakavyo shangaa nyinyi basi ndivyo jinsi nilivyo shangazwa hata na mimi pia”

Eddy akanyamaza kidogo huku akiwatazama viongozi wote kupitia tv hiyo kubwa na viongozi hao wote katika maeneo waliyopo nao pia wanamuona makamu wa raisi Eddy Godwin. Eddy akaminya moja ya batani ya laptop yake na kuruhusu video ya mauaji aliyo kuwa akiyafanya raisi Rahab kuonekana kwa kila mmoja wa wanaeshi hao kwenye tv yake huko alipo. Hapakuwa na hata mmoja ambaye aliwezza kuzuia mshangao wake, kila mmoja wasiwasi mwingi ukamjaa, kwa maana wanajeshi hao walikuwa wakiuwawa kikatili huku wengine wakivunjwa vunjwa baadhi ya viongo vya miili yao.

“Baada ya sote kuiona video hiyo, naamini kwamba nyote munaweza kwenda kufahamu nini kinacho kwenda kutokea. Hatuwezi kuendelea kuwa na uongozi wa raisi Rahab, kwa maana kwa sasa hatuelewi ni mtu ama shetani. Na naamini kwenye hiyo video muliniona na mimi pia nikishambuliwa, na kwa bahati nzuri tu sikuweza kufa kama walivyo kufa hao vijana wetu, wengi wao bado ni wadogo na wengine wana famillia zao”

“Kabla sijatoa maamuzi nitahitaji ushauri wenu”

Waziri mkuu akawa mtu wa kwanza kuomba kuzungumza na Eddy akamruhusu.

“Nashukuru muheshimiwa kwa kuweza kunipa nafasi ya kuchangia japo kidogo katika hilo. Hili ni swala la kushangaza sana. Ila kwa hali ya muheshimiwa raisi ilipo fikia kwa upande wangu nakuunga mmkono kwamba hafai kuendelea kuingoza hi nchi. Naamini kwamba madaraka yote sasa yapo chini yako”

“Okay nashukuru waziri mkuu. Ehee mkuu wa majeshi nakukaribisha?”

“Muheshimiwa kwa hilo lilo jitokeza kusema kweli limeniuma, japo sijajua hali hiyo imeanzia wapi kwa mama yetu raisi hapo, ila vifo vya vijana wetu vinaumiza sana. Tukiwa tunaendelea kuchunguza ni nini kinacho endelea kwake na mimi ninaunga mkono kwa sasa uchukua ikulu, ni hayo. Asanteni”

“Nashukuru mkuu wa majeshi. Sasa tunapiga kura ya kijeshi, nani anahitaji niwe raisi wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania?”

Wakuu wote wa kambi zote za jeshi wakakubai kunyoosha mikono yao juu.

“Nashukuru kwa kuniami. Kitu ambacho ninahitaji kukisisitizia kwa sasa ni kuhakikisha kwamba usalama wa nchi na wananchi unaimarishwa vya kutosha. Nimeeleweka?”

“Ndio muheshimiwa raisi”

“Kitu kingine hili jambo la kuugua kwa raisi Rahab ninaomba lisitoke nje, endapo mtu akabainika kwamba ametoa siri ya taifa na nina imani kwamba wote munafahamu kwa mkoasaji wa tukko kama hilo basi adhabu yake ni kuachia madaraka na atanyongwa hadi kufa. Nimeleweka waheshimiwa?”

“Ndio muheshimiwa raisi”

“Kikao kimekwisha”

Eddy alizungumza huku akinyanyuka kwenye kiti alicho kikalia.

“Niandalie helicopter naelekea ikulu Dar es Salaam. Mjulishe jaji mkuu na kukipambazuka tu nahitaji kuapishwa”

“Sawa muheshimiwa raisi”

Eddy akaongozana na Adrus kutoka katika chumba hicho.

“Nahitaji uwe mlinzi wangu namba moja na wakaribu kwa kipindi hichi kilicho bakia kuiongoza hii nchi”

“Sawa muheshimiwa”

Helicopter ikaandaliwa, Eddy na Adrus wakaingia katika helicopter hiyo ya jeshi na kuondoka kaktika eneo hilo la jeshi na kueleka ikuli Dar es Saalam.

***

K2 na kaka yake wakaendelea kupeana burudani huku undugu wakiwa wameutupa pembeni, kila mmoja akaanza kukiri kwamba anaridhishwa na mwenzake kwa kile ambacho amapatia.

“K2”

“Mmmmm”

“Kum** yako ni tamu sana”

“Kweli?”

“Yaa kweli?”

“Yaaa”

John alizungumza mara baada ya kumaliza kuburudishana na mdogo wake. K2 akanyanyuka kwenye sofa alilo kalia, akanza kutembe ataratibu hadi kwenye dirisha kubwa lililopo hapo sebleni na kufungua nje, mwanga mkali wa jua la asubuhi ukatawala ndani ya seble hiyo. Bwana John akachukua rimoti ya Tv yake na kuwasha ili kutambu kama wanatafutwa au laa.

“Hivi wanaweza kututafuta kweli?”

“Sidhani”

K2 alizungumza na kurudi alipo kaa kaka yake huku wote wawili wakiwa uchi kama walivyo zaliwa. Breaking News(Taarifa ya dharura) inayo onyeshwa na kitua cha chaneli ya taifa, ikawafanya K2 na kaka yake kukaa sawa kwenye sofa hilo kwani K2 alikuwa ameiweka miguu yake juu ya mapaja ya kaka yake huyo. ‘KUAPISHWA KWA

RAISI MPYA WA TANZANIA EDDY GODWIN KUTAWAJIA MUDA SI MREFU KUANZIA HIVI SASA’

Maandishi hayo yanayo pita taratibu sana kwenye kioo cha TV yao yakawanyong’onyeza sana kujikuta wakifikiria mambo mengi sana hususani juu ya kufa kwa raisi Rahab, ila kwa bahati mbaya hakuna kati yao anaye tambu ni kitu gani kilicho tokea.



“Eddy anaapishwa kuwa raisi…..!!?”

Bwana John aliuliza huku akiwa amejawa na mshangao mkubwa sana.

“Hata mimi mwenyewe sielewi”

***

“Phidaya, Phidaya amka njoo uone”

Shamsa alimuamsha Phidaya aliye lala kitandani huku akiwa amechoka sana kutokana na kuamka usiku ulio pita.

“Kuna nini?”

“Weee njoo tu uone”

Shamsa alizungumza huku akiwa amejawa na furaha kubwa sana usoni mwake. Phidaya akajifunga kitenge chake na kwa pamoja wakatoka chumbani humo na kuelekea sebleni na kuwakuta watu wote wakiwemo watu walimo ndani ya nyumba yao wakiwa wamekusanyika wakitazama tv kubwa iliyopo sebleni humo.

“Kuna nini?”

Phidaya aliuliza huku akitazama tv hiyo.

“Eddy anaapishwa kuwa raisi wa Tanzania”

“Kivipi?”

“Hata sisi hatufahamu”

Madam Mery alijibu kwa furaha huku akimtazama Phidaya usoni mwake. Wakamshuhudia Eddy akisimama kwenye moja ya kijukwaa katika viwanja vya ikulu huku kukiwa na viongozi kadhaa wakishuhudia tukio la kuapishwa kwa Eddy, kutoka kuwa makamu wa raisi hadi raisi wa Tanzania.

“Haiwezekani”

Phidaya alizungumza huku akiangaza huku na kule.

“Kwa nini sasa dada?”

Cookie naye aliuliza.

“Anaapishwaje ikiwa yupo raisi Rahab?”

“Na kweli”

Shamsa naye alichangia mada hiyo.

“Katiba ya nchi yoyote huwa makamu wa raisi anaweze kuchukua madaraka endapo raisi anapokuwa amekufa. Sasa munataka kuniambia kwamba Rahab amekufa?”

Swali la Phidaya likakosa jibu, mlango ukafunguliwa na wakaingia wanaume wanne walio valia suti nueusi, miwani nyeusi pamoja na vinasa sauti masikioni.

“First lady, unahitajika kuelekea ikulu hivi sasa, sisi ni walinzi wapya wa muheshimiwa raisi kutoka ikulu”

Mmoja wa walinzi hao alizungumza huku akimuangalia Phidaya usoni mwake. Phidaya akabaki akiwa amejawa na mshangao mkubwa sana.

“Jamani ni nini kinacho endelea?”

Phidaya aliuliza huku machozi yakimlenga lenga usoni mwake.

“Ndio hiyo umesha kuwa first lady wa Tanzania”

Shamsa alizungumza kwa furaha huku akimkumbatia Phidaya kwa furaha kubwa sana.

“Wifi yangu twende nikakuandae”

Madam Mery alizungumza huku akiwa amejawa na furaha kubwa sana. Wakamshika mkono yeye na Shamsa na kumpeleka hadi chumbani kwake.

“Nenda kaoge mama, au tukuogeshe?”

Madam Mery alizungumza huku akimshika Phidaya mkono wake wa kushota na kutaka kumuingiza bafuni.

“No ngoja tu nikaoge peke yangu”

Phidaya kaaingia bafuni huku hadi sasa hivi akiwa haamini kwa kile ambacho anakiona na kukisikia. Akaoga kwa haraka haraka huku akiwa na shauku kubwa sana ya kuhitaji kufahamu kwamab ni kitu gani ambacho kimemfanya mume wake kuwa raisi.

“Nimekuchagulia mahagauni hapa ni lipi linaweza kukufaa”

Shamsa alizungumza huku akimonyesha Phidaya magauni manne mazuri aliyo yaweka juu ya kitanda.

“Hilo jeupe”

“Hata mimi nilitaka kukuchagulia hilo jeupe”

Madam Mery alizungumza. Taratibu Phidaya akaanza kuvaa gauni hilo taratibu.

“Jamani mwenzenu mujue ninaona kama ni ndoto?”

“Sio ndoto ndio uhalisia, Eddy ndio amesha kuwa raisi sasa”

“Hata kama jamani ila Rahab atakuwa wapi.?”

“Muda wa sasa hivi sio wa kujiuliza Rahab yupo wapi, unacho takiwa sasa hivi ni kwenda ikulu mama”

Madam Mery alizungumza huku akiziweka nywele za Phidaya vizuri.

“Phidaya una ywele nzuri”

“Sisi mashombe shombe mwenzio si unamuona Shamsa naye nywele zake”

“Kweli, sisi nywele zetu hadi tuangaike na madawa ya kuzilainisha”

“Hahaa”

“Shamsa utawaangalia watoto wote nina imani baadae nanyi mutafatwa”

“Yaa”

Wakatoka chumbani humo. Kila mtu sebleni akamsifia Phidaya na kumuambia kwamba amependeza. Phidaya akachukuliwa na walinzi hao wa ikulu, wakaingia kwenye gari aina Cadillac Escalades magari yanayo tengenezwa kwa uimara ubora wa kuto shambuliwa kwa anamba yoyote ile pasipo watu waliomo ndani ya gari hilo kuudhurika. Na ubora mwengine wa gari aina hiyo ni kuto kuingia risasi wala bomu kuweza kulilipua. Taratibu gari hizo mbili za kisasa zikaanza kuondoka katika jumba hilo huku Phidaya akiwa amekaa siti ya nyuma huku dereva na mlinzi mmoja wakiwa wamekaa siti ya mbele. Kitendo cha kutoka uzio wa jumba hilo madereva wakawasha ving’ora vya kuweza kuwaashira madereva wengine kuweza kupisha njia, kwani ndani ya gari hilo kuna mtu muhimu kwa sasa hapa Tanzania.

“Samahani ninaweza kuuliza swali?”

Phidaya aliuliza huku akimtazama mlinzi huyo.

“Ndio madam”

“Imekuwaje kuwaje mume wangu akawa raisi?”

“Madam kwa mimi siwezi kukupa jibu sahihi, mimi ni mlinzi na ninatekeleza majukumu yangu ya ulinzi tu”

“Sawa”

Kwa kasi ya gari hizo na kupishwa barabarani na madereva wengine. Wakafanikiwa kufika ikulu ndani ya muda mchache sana. Rahab akapokelewa na walinzi wawili wa kike walio valia suti nyeusi huku nao wakionekana ni watu hatari sana katika swala zima la ulinzi.

“Twende huku madam”

Mmoja wao alizungumza huku akitangulia mble na mwengine akimfwata Phidaya nyuma yake. Wakaingia kwenye ofisi ya raisi na Phidaya akashuhudia picha kubwa ya mumewe ikiwa imebadikwa kwenye moja wa ukuta wa ofisi hiyo huku ikiwa na maandishi meusi chuni yake yanayo someka ‘Eddy Godwin. Raisi wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania’

“Muheshimiwa raisi atakuja hivi sasa”

“Sawa”

Walinzi hao wakatoka ndani ya ofisi hiyo na kumuacha Phidaya peke yake akiendelea kushanga shangaa ofisi hiyo. Baada ya dakika kama ishirini hivi mlango ukafunguliwa na akaingia Eddy akiwa na furaha sana. Kwa haraka Phidaya akimbilia mume wake na kumkumbatia kwa nguvu huku wakimwagikwa na machozi ya fura.

“Mke wangu nimekuwa, nimekuwa raisi mke wangu”

Eddy alizungumza huku machozi yakiendelea kumwagika. Kilicho hicho cha furaha kikamzisha Phidaya kulia kwa uchungu na kupata kigugumizi cha kumjibu mume wake juu ya hilo jambo alilo lizunguma. Taratibu Eddy mshika Phidaya mashavu yake na tartaibu wakaanza kunyonyana midomo yao kwa dakika kama mbili hivi kisha wakaachiana.

“Phidaya”

“Bee mume wangu”

“Tumefanikisha ndoto zako, ulinihitaji niwe raisi na nimefanikiwa kuwa raisi mke wangu”

Phidaya akamkumbatia tena mume wake kwa nguvu sana na kuendelea kumwagikwa na machozi ya furaha. Hisia ya furaha kali iliyo watawala ikadumu kama dakika kumi hivi kisha kila mmoja akamuachia mwenzake.

“Phidya mke wangu”

“Mmmmm”

“Hii kazi ni ngumu, peke yangu sinto weza kuifanya. Nahitaji wewe ndio uwe mshauri wangu wa mwisho katika kila jambo, tafadhali ninakuomba mpenzi wangu ukubaliane nami katika hilo”

“Mume wangu, wewe ndio mkono wangu wa kulia, mimi nimetoka kwenye mbavu zako za kushoto. Ukiumia wewe basi nami nina umia. Nipo tayari kukesha nawe, nipo tayari kwenda popote nawe ili mradi niweze tu kukusaidia kuingoza hii nchi. Natamani sana siku moja ukiachia madaraka basi watu wakukumbuke kwamba ulikuwa ni kiongozi mwema na bora”

Phidaya alizungumza kwa sauti ya upole na iliyo jaa mahaba ya kimapenzi ndani yake.

“Nashukuru mke wangu, sijuti kuwa nawe”

“Hata mimi baba Junion sijutii kuwa nawe”

***

Si Watanzania tu walio jawa na mshangao wa kuamka asubuhi na kukuta makamu wa raisi akiapishwa, bali hata John adui mkubwa wa Eddy alijikuta akijawa na mshangao na mipango yake yote alio kuwa ameipanga kwa ajili ya kumuangamiza Eddy ikaharibika.

“Muheshimiwa Dumbe anapiga simu”

Mlinzi wa karibu wa John alizungumza huku akiwa ameishia simu aina ya iphone 7 mkononi mwake. John akatazama tv kubw ainayo oyesha taarifa ya habari kutoka shirika la utangazaji la BBC nchini Uingereza, kuhusiana na Tanzania kupata raisi mpya ambaye ni bwana Eddy Godwin, mtoto wa aliye kuwa mzee Godwin raisi aliye pinduliwa nchini Tanzania.

“Muheshimiwa”

“Waambie kwamba sipo”

John alizungumza kwa upole huku akiwa amechoka sana. Mlinzi wake huyo akatoka na akabaki peke yake.

‘Eddy kweli ni chaguo la Mungu sinto weza kupambana naye’

John alijikuta akikiri moyoni mwake juu ya tukio hilo, kwani hakuwahi kufikiria kwamba ipo siku moja rafiki yake huyo wa kipindi kirefu toka walipokuwa wanasoma shule ya sekondari.

“Hahahaa, Eddy kweli wewe ni mshenzi. Eddy wewe ni mshenziiii”

John alizungumza kwa uchungu sana ulio ambatana na kuchela huku mkononi mwake akishika chupa ya pombe kali na kuanza kunywa mafumba kadhaa ili kuhakikisha kwamba anakiweka kichwa chake sawa.

“Heii”

John alimuita mlinzi wake.

“Ndio mkuu”

“Nitafutie malaya wawili wazuri sana nahitaji kuwa nao usiku mzima wa leo”

“Sawa muheshimiwa”

John akaendelea kujilaza kwenye sofa hilo hukua akiwa amekata tamaa kabisa kwani hana pesa ya kupambana na Eddy, pili Eddy tayari kwa sasa amekuwa ni raisi ambaye naamini ulinzi utazidi kuimarishwa kwenye nchi yake na ili kuweza kumfikia yeye basi ni jambo gumu sana ambalo linaweza kugarimu maisha ya watu wengi sana.

***

Ulinzi mkali ukaendelea kuimarishwa katika chumba alicho fungiwa raisi Rahab ambaye, kila mwanajeshi hivi sasa anatambua uhatari wake kwani mauji mengi aliyo yafanya wa wezao kila mmoja ana wasiwasi naye. Majira ya saa nne asubuhi, Rahab akafumgua macho yake huku akihema sana, akajitazama mwili wake jinsi ulivyo choka na kujawa na maumivu ya hapa na pale. Taratibu akaanza kuchunguza chumba alicho alicho lazwa. Akasimama na kutembea hadi mlangoni, akafungua kidirisha kidogo cha chumba hicho na kuwaona wanajeshi wawili wakiwa wamesimama nje ya mlango huo.

“Heiii”

Rahab aliita kwa sauti ya upole na unyonge mwingi sana jambo lililo wastua wanajeshi hao.

“Hei mbona mumenifungia humu ndani, kuna nini kinacho endelea?”

Wanajeshi hawa wakajikuta wakitetemeka sana kwa woga, kwani yule mtu waliyekuwa wakimuona kama shetani hapa anazungumza kwa sauti ya upole na unyonge mwingi sana ndani yake.

“Jamani si ninawauliza jamani”

“Samahani muheshimiwa hupaswi kutoka nje kwa sasa”

“Kwa nini?”

“Aha…..unajua….”

“Nifungulieni”

“Hapana muheshimiwa hauwezi kutoka sasa hivi”

“Ahaa…kwa hiyo mumeniteka raisi wenu si ndio?”

Rahab alizungumza kwa ukali kidogo na kuzidi kuwachanganya wanajeshi hao.

“Sasa hii ni amri ninawamrisha kama raisi wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania, fungueni mlango huu na ole wake yule anaye pinga amri yangu nitamchukulia kama msaliti kwenye serikali yangu sawa”

Maneno makali ya Rahab yakazidi kuwapa woga wanajeshi hawa wawili ambao ni vijana tu wadogo na ndio kwanza wana mwaka mmoja jeshini. Vijana hao wakashauriana kwa macho na kujikuta mmoja wao akianza kushika kitasa na kukifungua taratibu, jambo lililo mfanya Rahab kutazama pembeni huku akitabasamu na macho yake yakarudi kwenye hali ya uwekundu unao ashiria kwamba amerudi kwenye hali yake ile ile ya hasira kali inayo pelekea mauji mabaya kwa yoyote ambaye atasimama mbele yake.



Mwajeshi huyo kabla hajafika mwisho wa kufungu kitasa cha mlango wa kitasa hicho, sauti kali ya kumuonya ikasikika. Kwa haraka mwanajeshi huyo akajikuta kwamba akisitisha zoezi hilo na kupiga saluti kwa mkubwa wake huyo aliye weza kufika katika eneo hilo.

“Munafanya nini nyinyi, muna akili kweli?”

Mkubwa huyo alizungumza huku akiwahi kwenye mlango huo na kufunga kitasa hicho vizuri.

“Usiwafokee mimi ndio nimewaamuru wafungue mlango huo”

Rahab alizungumza kwa sauti ya upole sana huku akimtazama mkuu huyo wa kambi ya jeshi. Mkuu wa jeshi tofauti na alicho kifikiria kumuona nacho Rahab ni tofauti kabisa na hichi anacho kiona kwani Rahab anazungumza kwa upole na unyonge sana kana kwamba sio yule alite kuwa amefanya mauaji ya jana usiku kwenye kambi hiyo.

“Muheshimiwa”

“Beee”

“Upo sawa lakini?”

“Ndio, natambua kwamba wengi wenu munaniogopa ila nipo sawa sasa”

“Ila sahamani sana muheshimiwa, sina ruhusa ya kukufungulia humo ndani hadi kutoka kwa raisi”

“Kutoka kwa raisi, raisi yupi?”

“Eddy, asubuhi ya leo amepishwa na kuchukua nafasi yako, hii yote ni kutokana na hali yako ya jana usiku”

“Una namba yake ya simu hapo?”

“Ndio”

“Naomba nizungumze naye”

Mkuu huyo wa jeshi akajishauri kwa sekunde kadhaa, ila kutokana zungumza ya Rahab ni ya kistarabu kama vile alivyo kuwa madarakani, hakuona haja ya kuleta kipingamizi cha aina yoyote. Akatoa simu yake mfukoni, na kuitafuta namba ya raisi Eddy na kumkabidhi Rahab.

“Hiyo hapo muheshimiwa”

“Umesema kwamba amesha apishwa?”

“Ndio”

Rahab akaipiga namba hiyo na kuiweka sikioni mwake. Simu ya Eddy ikaanza kuita taratibu.

***

Eddy akajipapasa kwenye mfukono wake wa koti na kuitoa simua kea mfukoni. Akakuta namba ya mkuu wa kambi ya jeshi mkono Morogoro ndio anaye mpigia.

“Kaa hapo”

Eddy alimuambia Phidaya huku akizunguka meza na kukaa katika kiti kilichopo nyuma ya meza hiyo. Akapokea simu yake hiyo na kuiweka sikioni.

“Halooo”

Eddy alianza kuzungumza ila ukimya mzito ukatawala katika upande wa pili wa simu hiyo jambo lililo mfanya arudie tena kuzungumza neno hilo hilo ila hakuweza kusikia chochote.

“Eddy”

Sauti ya Rahab ikamstua sana Eddy na kujikuta akikaa vizuri kwenye kiti chake kiasi kwamba hata Phidaya akafahamu mstuko wa mume wake.

“Eddy”

“Mmmmm”

“Nashukuru sana kwa hichi ulicho kifanya, natambua kwamba nimekuwa ni mtu mwenye hasira, hasira ambayo inakuwa ni mbaya kwa kila mtu. Nakuomba unisamehe kwa kila kibaya nilicho kufanya. Naomba usimueleze mtu juu yangu, najua ni wangu wengi sana watahitaji kuhoji kwa kile ambacho kimetokea leo cha wewe kuapishwa kuwa raisi pasipo habari yoyote ya kuhusiana na mimi”

Eddy akashusha pumzi nzito huku akimtazama mke wake na jasho taratibu likaanza kumwagika usoni mwake.

“Eddy waongoze Watanzania katika misingi ya kisheria, haki. Futa makosa aliyo yafanya baba yako, hakikisha kwamba kila mmoja anapenda uongozi wako sawa”

“Sawa”

“Kitu kingine nahitaji kukuona kwa mara ya mwisho, nahitaji joto lako kwa mara ya mwisho. Nakuomba leo uje huku Morogoro, nakuomba sana uweze kufika leo sawa mpenzi wangu”

“Nimekuelewa”

“Kitu kingine……au basi ukija huku nitazungumza nawe baadae”

Simu ikakatwa, Eddy taratibu akaitazama simu yake hiyo kisha akaiweka juu ya meza yake na kujifuta jasho kwa kutumia kiganja chake cha mkono wake wa kulia. Phidaya akanyanyuka taratibu kwenye kiti chake akazunguka katika upande wa pili alipo kaa mume wake, akatoa kitambaa kidogo kinacho nukia vizuri kwenye pochi yake ndogo, taratibu akaanza kumfuta Eddy jasho hilo linalo mwagika usoni mwake lililo sababishwa na hofo pamoja na wasiwasi mwingi.

“Mume wangu”

“Ndio mke wangu”

“Natambua kwamba una wasiwasi mwingi sana na hii kazi. Pia natambua kwamba hii kazi ni ngumu sana, ila nakuomba usiwe na wasiwasi mume wangu, gumu lako ni gumu langu, nakuomba uwe unanieleza kila kitu ambacho kwako inahisi ni kigumu kukibeba moyoni mwako wewe mwenyewe. Tambua kwamba ninakupenda na ninahitaji kuwa mke bora kwako”

Maneno ya Phidaya aliyo yazungumza kwa sauti ya upole na iliyo jaa mahaba mazito yakamfanya Eddy kufarijika sana.

“Nimetoka kuzungumza na Rahab”

“Rahab?”

“Ndio, Rahab jana usiku kuna siri kubwa sana ambayo sikuwahi kuitambua kwenye maisha yake, siri ambayo imepelelea hadi mimi kuchukua madaraka haya ya kuiongoza nchi”

“Ni siri gani hiyo?”

Eddy akamtazama Phidaya usoni mwake, kisha taratibu akamshika kiuno na kumkalisha kwenye paja lake la mguu wa kulia.

“Niahidi utanifichia siri, kwa sababu wewe ni mke wangu”

“Nitaificha siri yoyote ambayo utanieleza kama mke wako, na hata iweje sinto muambia mtu wa aina yoyote niamini mume wangu”

‘……naomba usimueleze mtu juu yangu……….’

Kauli hiyo ya Rahab aliyo toka kuizungumza muda mchache ulio pita ikakatiza kichwani mwa Eddy kwa kasi ya ajabu kubwa sana na kujikuta akipata kipingamizi cha kumuambia Phidya kitu kile alicho kuwa amekikusudia kukizungumza.

“Tutazungumza baade mke wangu nikitoka mkoni Morogoro”

“Eddy…..”

“Ndio mke wangu tutazungumza baade sawa mama watoto?”

“Sawa mume wangu kama ni hivyo”

“Sasa hivi nitakukabidhi kwa muangalizi wa ikulu, atakutembeza katika maeneo yote ya hapa ikulu sawa”

“Sawa mume wangu”

Eddy akanayua mkonga wa simu yake na kumpigia sekretari wake na kumuomba aweze kufika ofisini humo, akampa maelezo ya mke wake jinsi anavyo takiwa kuweza kuonyeshwa mazingira ya eneo hilo la ikulu kwani wanakwenda kuishia katika ikulu hiyo kw amiaka kadhaa kabla ya uchaguzi mkuu kufika.

***

“K2”

Bwana John aliita huku akimtazama mdogo wake ambaye hadi sasa amejawa na bumbuwazi la kujiuliza imekuwaje hadi Eddy kuapishwa kuwa raisi wa Tanzania.

“Mmmm”

“Tuna nafasi yakuingia madarakani”

“Nafasi ya kuingia madarakani?”

“Ndio”

“Ipo wapi hiyo nafasi ikiwa mtu aliye shika madaraka ni mtu ambaye hatumjui vizuri na historia yake tu inaonyesha kwamba ni mtu asiye penda masihara?”

“Naamini kwamba Eddy Godwin anaweza kwenda kutengeza demokrasi, anaweza kwenda kuiweka nchi hii katika usawa wa haki. Tujipange kisiasa sasa kwa maana hadi sasa ni damu za watu wengi sana zimeweza kumwagika tena watu walio kuwa kwa upande wetu. Hatuwezi kuendelea kupoteza maisha ya vijana wadogo wenye ndugu zao, wengine familia zao kwa uchu wa madaraka yetu sisi wawili.”

Bwana John alizungumza kwa msisitizo huku akimtazama K2 usoni mwake.

“Unahisi kusimama jukwaani inaweza kutosha na kutupa nafasi wewe kuingai mdarakani?”

“Ndio, kama pesa ninayo, hivi sasa cha kufanya ni kuhakikisha kwamba ninakuwa ndani ya serikali. Kwa maana nina imani kwamba raisi atachangua utawala uliopita kwa baadhi ya nafasi na lile pendekezo lako la kufungua kituo cha usalama ambacho kitakuwa kinashuhulikika maswala yote yanayo husiana na ugaidi na kesi zile ngumu, ndio mua wake wa kwenda kukianzisha”

“Sawa kama wewe mwenyewe unahitaji tutumie akili nyingi katika hili, basi hakuna shaka wa maana vita yote tunayo ipigana muda huu ni kwa ajili yako wewe”

“Nashukuru kwa kunielewa mdogo wangu”

“Sawa ila kitu kingine yule rafiki yako ulite msaidia kumtorosha, wasiliana naye ili ikiwezekana tuwekeze pesa yetu ili huko mbeleni tukihitaji msaada basi wake basi inakuwa raisi”

“Sawa nimekuelewa, tena kama inawezekana ngoja niwasiliane naye sasa hivi”

K2 akaichukua simu yake na kumpigia Livna Livba. Simu ya Livna ikapokelewa.

“Ni mimi”

“Niambie best naona nchini mwako kiongozi amebadilika, vipi kiongozi aliye pita mumemfanyia umafia nini?”

“Hapana, jinsi unavyo shangaa wewe ndiyo jinsi ninavyo shangaa mimi. Ila hakuna kilicho haribika”

“Unataka kuniambia kwamba hufahamu alipo raisi aliye pita?”

“Ndio mara ya mwisho kuonana naye ni jana usiku. Ila mambo hayo tuachane nayo, nahitaji kufanya kitu juu ya kikosi chako”

“Kitu gani?”

“Nahitaji kuwekeza kiasi cha pesa katika kikosi chako je inawezekana?”

“Hahaa…..K2 una pesa kweli ya kuwekeza kwangu?

“Wewe niambie tu ni kiasi gani ambacho unahitaji niwekeze kwako?”

“Dola bilioni ishirini, kwa maan hicho ndio kiasi ambacho ninaweza kukuambia uweze kuwekeza kwangu”

“Sawa nitakupatia hicho kiasi”

“Una uhakika K2 una hicho kiasi?”

“Ndio kwa nini una wasiwasi gani, si nikishindwa si nitaacha kufanya hilo jambo”

“Sawa ninakukaribisha sana”

“Nashukuru”

“Lini siku ya kukutana?”

“Nitakuambia”

K2 akakata simu na kumtazama kaka yake.

“Anasemaje?”

“Anahitaji kiasi cha dola bilioni ishirini za Kimarekani”

“Sawa, nitatoa kiasi hicho kutoka kwenye kampuni zangu za migodi kisha baada ya hapo nitakupatia ili muweze kufanya makubaliano, hakikisha kwamba unakuwa na nguvu katika kikosi hicho kutokana na pesa ambayo ninakupatia”

“Usijali kaka yangu”

***

Mara baada ya Phidaya kutoka katika ofisi yake. Eddya katoa kitabu alicho kabidhi na dokta William, akaanza kukifungua karatasi kadhaa huku akitafuta sehemu alipo kuwa ameishia kusoma. Akakutana na maandishi ambayo yanayosomeka. ‘MBINU ZA KUMUUA RAHAB’ . Akataka kuzisoma ila mlango wake ukagongwa na kujikuta akikifunika kitabu hicho na kumruhusu mtu anaye gonga mlango huo. Akiingia Adrus, akamkaribisha huku akiwa amejawa na tabasamu pana usoni mwake.

“Ofisi imekufaa muheshimiwa”

“Etii ehee?”

“Ndio muheshimiwa. Muheshimiwa ninaomba ruhusa niende hotelini kuonana na Naomi kwa maana toka nilipo muacha jana nahisi huko atakuwa na wasiwasi mwingi sana”

“Okay sawa, ila uwahi kurudi kwa maana nahitaji kwenda Morogoro kuonana na Rahab”

“Rahab?”

“Ndio, amezungumza nami leo ila nahitaji kwenda kumuua kwa maana sihitaji kumuona tena duniani, anaweza kusababisha mauaji mengi zaidi ya yale aliyo yafanya jana”

“Muheshimiwa utamuua vipi ikiwa hata akipigwa risasi hafi?”

Eddy akamtazama Adrus kwa muda kisha akakishika kitabu alicho pewa na dokta William.

“Mbinu zaote za kumuua Rahab zipo humu, nitazisoma na kuhakiksiha ninamuua leo hii hii”

Eddy alizungumza kwa msisitizo huku akikipiga piga kitabu hicho jambo alicho kishika.



“Muheshimiwa una uhakika kwamba mbinu zilizo andikwa ndani ya hicho kitabu zinaweza kufanya kazi?”

“Asilimia mia moja nina unahakika nazo”

“Tuangalie isije ikawa ni blablaa za yule daktari”

“Amini hilo”

“Sawa, ila naomba nitekeleze ombi langu nililo kuomba”

“Sawa nenda muda wa saa kumi na mbili jioni uwepo hapa kwa maana safari itakuwa ni usiku”

“Nashukuru muheshimiwa”

Adrus akasimama kwenye kiti alicho kikalia, akatoka ndani ya ofisi hiyo huku nyuma akimuacha Eddy akianza kusoma mbinu hizo zilizo andikwa na dokta William. Adrus akaingia kwenye gari aliko kabidhiwa na mkurugenzi wa ikulu. Moja kwa moja akaelekea hadi ilipo hoteli ambayo alimuacha Naomi. Akasimamisha gari lake kwene maegesho maalumu, kisha akatoa simu yake mfukoni, akaitazama kwa muda kisha akaitafuta namba ya mama yake na kumpigia. Simu ya mama yake haikumaliza hata sekunde kumi katika kuita ikapokelewa.

“Ndio mama”

“Adrus mwanangu upo wapi?”

“Nilikuwa ikulu mama, ila sasa hivi kuna kitu ambacho nahitaji kukuambia japo ni suprize”

“Kitu gani?”

“Nipo hotelini na Naomi”

“Naomi yupi. Yule mpenzi wako?”

“Ndio mama yangu”

“Msalimie”

“Ila mbona kama unaonekana kama hujawa na furaha ya kutosha”

“Hapana mbona nina furaha”

“Mama”

“Kweli”

“Apia kwa mwenyezi Mungu kama upo vizuri”

“Adrus, roho yangu inaniuma sana”

“Kwa nini, furahi mama nipo na mwanamke ninaye mpenda”

“Najua hilo, ila najisikia vibaya sana kuona Cookie anashindwa kula, anashindwa kufanya kazi zake zoete yote kwa ajili yako. Tafadhali nakuomba ufanye jambo juu ya hili kwa maana hapa nyumbani kila mmoja yupo upande wa Cookie na jana kutwa nzima mtoto wa watu ameshinda akiwa analia. Tafadhali A drus fanya jambo juu ya hilo swala, sawa baba yangu”

“Ila mama……”

“Najua kwamba unampenda sana Naomi, ila kumbuka kuna mwanamke mwengine kama mama yako, analia, anashindwa kula anahuzuni muda wote. Jaribu basi kufanya japo usamaria mwema kwake”

Adrus akashusha pumzi mara baada ya kuyasikiliza maneno ya mama yake yaliyo jaa hekima nyingi ndani yake.

“Dini, dini yetu inaruhusu kuwa na hata wake wanne . Ila nakuomba mimi uweze kuwafanya mpango wa kuwao hao wawili tu. Nipo chini ya miguu yako kwa maana najua Naomi anakupenda na unampenda, ila pia Cookie anakupenda na una chembechembe za kumpenda pia. Tafadhali ninakuomba sana uweze kuwa na hawa mabinti la zivyo tunaweza kwenda kuwapoteza mmoja wao na wafanye wapendane. Sawa Adrus mwanangu?”

“Sawa mama nimekuelewa”

“Unarudi nyumbani saa ngapi?”

“Muda si mrefu”

“Basi fanya urudi na huyo Naomi”

“Sawa mama yangu”

Adrus akakata simu huku akijiuliza maswali mengi yasiyo na majibu juu ya kubadilika huku kwa msimammo wa mama yake. Akafungua mlango wa gari lake na kushuka, moja kwa moja akaelekea kwenye chumba alipo muacha Naomi. Akaminya kitufe cha kengele kilichopo pembezoni mwa mlango huo. Hazikupita dakika nyingi, Naomi akafungua mlango huo huku bastola yake akia wamificha kwa nyuma. Alipo kuta ni Adrus kwa haraka akamkumbatia huku akimpiga mabusu mfululizo usoni na mdomoni mwake. Adrus akaufunga mlango huo, kisha taratibu akaanza kutembea huku Naomi akiwa amembembea mwilini mwake, akamlaza kitanda na wakaendelea kunyonyana midomo yao.

“Pole kwa majukumu mume wangu”

“Nashukuru mke wangu”

Adrus alizungumza huku akimuachia Naomi kisha akaka kitako kitandani, akaanza kufungu vifungo vya shati lake pamoja na tai yake.

“Nakuomba nikusaidie”

“Sawa”

Naomi akanza kumvua Adrus koti la suti taratibu, kisha akafwatia tai yake na kumalizia shati hilo lililo mbana Adrus vizuri mwilini mwake na kumfanya azidi kuonekana mtanashati kutokana na mwili wake mazoezi.

“Baby”

“Mmmmm”

“Leo nahitaji twende ukamuone mama”

“Adrus…..!!”

Naomi aliita huku akiwa ametawaliwa na mshangao mkubwa sana.

“Ndio, mbona umeshangaa?”

“Siamini kama umeweza kunifanyia suprize ya namna hii mpenzi wangu”

“Yaa, nahitaji umuone mama aliye mzaa kijana ambaye unapenda kuliko chochote”

Kwa haraka Naomi akamkumbatia Adrus huku machozi yakimwagika usoni mwake, kwani hadhi aliyo kabidhiwa na Adrus ni hadhi kubwa sana ambayo kwenye maisha yake hakuwai kuipata kwa mwanaume wake wa kwanza.

“Nakupenda sana Adrus”

“Nakupenda pia mke wangu, nakupenda sana Naomi wangu, tafadhali ninakuomba usiniache mpenzi wangu”

“Adrus siwezi kufanya kitu kama hicho mpenzi wangu ninakuomba uniamini”

“Sawa, ila kuna ombi moja ambalo maama ameniomba”

“Ombi gani hilo mpenzi wnagu”

Adrus akaka kimya kwa muda huku akimtazama Naomi usoni mwake. Taratibu Adrus akajilaza chali kitandani na kumfanya Naomi naye kujilaza pembeni yake huku kichwa chake akiwa amekilaza juu ya kifua cha Adrus.

“Baby niambie mume wangu ni ombi gani ambalo mama amekuaomba jamani”

“Mama ameniaomba niweze kuwaoa wewe na yule msichana muliye gombana jana kisa mimi. HIi yote ni kutokana munanipenda na kila mmoja ana haki ya kuwa nami”

Naomi taratibu akanyanyua kichwa chake na kumtazama Adrus usoni mwake pasipo kuzungumza kitu cha aina yoyote.

***

Mama Adrus taratibu akashuka kitandani mwake huku akiwa na shauku ya kuzungumza kitu na Cookie, msichana anaye amaini kwamba amemkosea kwa kiasi kikubwa sana. Mama Adrus akajifunga kitenge chake vizuri na kutoka chumbani kwake humu. Akakutana na Sa Yoo kwenye kordo, wakasalimiana na Sa Yoo akaingia kwenye chumba chake. Mama Adrus akaelekea sebleni na kuwakuta watu wakiwa wamekaa kwenye sofa huku wakiwa anajadiliana mada ambayo haifahamu. Wenye umri mdogo kwa mama Adrus wakamsalimia akiwemo Cookie na wenye umri sawa naye au wanaye karibiana naye kama Madam Mery wakasalimiana tu kawaida.

“Mama Eddy amekuwa raisi”

Cookie alizungumza kwa furaha huku akimtazama mama Adrus usoni mwake.

“Amekuwa raisi?”

“Ndio, ametoka kuapishwa kama lisaa moja na nusu hivi lililo pita”

“Jamani ni kweli?”

Mama Adrus alijikaza kumtazama kuzungumza huku akimtazama Jing ambaye anakumbuka ni kitu gania mbacho alifanywa siku ya jana.

“Ni kweli”

“Raisi wa sasa hivi amejiudhuru?”

“Hakuna anaye fahamu hadi sasa hivi na kila mtu anasubiria kauli ya kufahamu ni nini kilicho mpata raisi wa sasa hivi”

“Sawa sawa. Jamani kuna jambo ambalo ninaomba nilizungumze na wote muweze kulisikia”

Mama Adrusa alizungumza kwa sauti ya upole na kuwafanya watu wote ndanii ya seble hii kuka kimya huku wakihitaji kusikia nikitu gani ambacho anahitaji kukizungumza.

“Nina imani kwamba sisi sote ni wanawake tulipo humu ndani na nina imani kwamba muna fahamu maumivu ya mapenzi si ndio?”

“Ndio tena mimi ninayafahamu sana kwa maana yalitumbisha maisha ya raisi wetu huyu wa sasa tunaye mshangilia”

Madam Mery alizungumza kwa msisitizo.

“Samahani mama Adrus kwa kukukatisha unacho hitaji kukizungumza. Ehee madam Mery, mapenzi yaliyumbishaje maisha ya raisi wetu wa sasa hivi?”

Lee Ji aliuliza huku akimtazama madam Mery usoni mwake.

“Ngoja mama azungumze kisha nitawaadisia na mimi”

“Zungumza tu kwa maana naamini itaonyesha picha katika hichi nilicho panga kukizungumza.”

Maneno ya mama Adrus yakamfanya Cookie mapigo ya moyo kuanza kumuenda mbio kiasi cha kushindwa kabisa kustahimili na mwili mzima ukaanza kumtetemeka.

“Vipi mbona una tetemeka?”

Shamsa aliuliza makusudi huku akimtazama Cookie ambaye amepoteza amani na furaha kabisa kwa maana anamini kwamba maneno ya mama Adrus anayo kwenda kuyazungumza ni kumkataa mbele ya watu wote hapo sebleni. Cookie akasimama na kuanza kutembea ili kuondoka eneo hilo.

“Cookie”

Mama Adrus alimuita huku akisimama. Cookie mapigo ya moyo yakazidi kumuenda kasi na kujikuta akisimama na kushindwa kabisa kugeuka nyuma kwani anatambua jibu litakalo toka hapo ni kumkosa Adrus.

“Natambua kwamba unampenda sana mwanangu, natambua kwamba umefanya mambo mengi sana na mwanangu Adrus. Nikiwa kama mama yake mzazi natambua kwamba nilikumtakia maneno mabaya jana ambayo hukukusudia kuweza kuyasiki kutoka kinywani mwangu kama mama”

Mama Adrus alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake.

“Nayajua maumivu ya mapenzi, najua jana siku nzima hukula yote ni kwa ajili ya mwanangu. Ninakuomba sana uweze kunisamehe, nakuomba sana uweze kutambua kwamba mama mkwe wako nilikukosea sana. Nipo tayari Adrus mwanangu akuoe”

Taratibu Cookie akageuka na kumtazama mama Adrus kwa macho yaliyo jaa mshangao mkubwa sana huku na yeye machozi yakiwa yanamwagika usoni mwake.

“Karibu kwenye familia yangu, karibu kwenye familia ya bwana Maldin.”

Mama Adrus alizungumza hukua akiitanua mikono yake kwa ishara ya kuhitaji kumkumbatia Cookie. Cookie kwa haraka akamkimbilia mama Adrus na kumkumbatia kwa nguvu huku wote wakiangua kilio kizito kilicho jaa hisia kali na furaha.

Kila aliyomo hapo sebleni, kitendo hicho walicho kifanya mama Adruds na Cookie, kiwawafanya kulengwa lengwa na machozi kwenye macho yao. Taratibu Shamsa akanyanyuka katika sehemua aliyo kaa na kuwasohelea mama Adrus na Cookie, kwa pamoja akawakumbatia kwa nguvu.

“Nashukuru sana mama Adrus”

Shamsa alizungumza.

“Nashukuru nawe Shamsa. Ila nimezungumza na Adrus”

Mama Adrus alizungumza huku akiwaachia Cookie na Shamsa na kuwafanya watu wote watege measikio yao kwa umakini kumsikiliza ni kitu gani ambacho anahitaji kukizungumza kwa muda huu.

“Adrus nimemuaomaba kitu kimoja kama mama yake. Natambua kwamba anampenda Cookie na pia anampenda Naomi msichana ambaye yupo naye. Nimemuomba aweze kuwaoa wote wawili kutokana dini yetu ya Kiislam inaruhusu kwa mwanaume mmoja kuweza kuoa wanawake wanne”

“Yote heri mama, mimi nipo tayari kuwa hata mke wa pili. Ninampenda sana Adrus yeye ndio mwanaume wa ndoto zangu, yeye ndio baba yangu, yeye ndio kila kitu kwangu. Sina sehemu nyigine ya kwenda zaidi ka kuwa mkewe hadi mwisho wa maisha yangu”

Cookie alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake. Watu wote ndani ya hii seble wakapiga makofi ya kumpongeza Cookie kwa maamuzi yake ya kuamua kuuweka wivu pembeni na kuangalia hisia zake za moyo zinahiyaji nini kwa sasa.

“Haya sasa jamani madam Mery endelea na hadithi yetu juu ya Eddy”

Shamsa alizungumza huku akirudi kwenye sofa alilokuwa amekaa.

“Wee muambieni awasimulie yeye mwenyewe, sitaki kusutwa jamani”

“Jamani”

“Adisia, Adisia, Adisia”

Jing alianzisha wimbo huo na kumfanya Shamsa kujumuika katika kuuimba wakimsisitiza madam Mery aweze kuuadisia huo wimbo.

“Jamani, haya musiimbe nawaadisia”

Madama Mery alizungumza huku akiwa amejawa na furaha kubwa sana. Akaanza kuwaadisia kila kitu ambacho alikifanya maisha ya nyuma ya Eddy pasipo kuficha kitu chochote toka alipokuwa mwalimu hadi walipo fikia hivi sasa.

***

“Naweza kwenda maabara”

Dokta William alizunumza mara baada ya daktari kuingia katika chumba alicho lazwa mara baada ya kuhudumiwa juu ya jeraha lake alilo pigwa risasi.

“Hali yako haijakaa vizuri, unatakiwa upumzike sana”

“Hapana, kuna kitu ninahitaji niweze kukifanya ni muhimu sana”

Daktari akafikiria kwa muda kisha akakubaliana na dokta William. Akamasaidia kumshusha kitandani na kumkalisha katika kiti cha matairi na kuanza kumsukuma taratibu na kuelekea katika maaabara ya hospitali hiyo. Wakiwa njiani wakakutana na mkuu wa kambi hiyo. Mwanajeshi huyo akapiga saluti kama iliyo kawaida ya wanajeshi wote endapo wanakutana na mkuu wao.

“Vipi maendeleo yako dakatri?”

“Salama tu, ninahitaji kuelekea maabara kuna dawa nahitaji kuitengeneza ni muhimu sana”

“Ahaa….sawa uwanja ni wako na pia raisi amerudi katika hali yake ya kawaida?”

“Hali yake ya kawaida?”

“Ndio, mida ya asubuhi nilikwenda kuzungumza naye na amezungumza na raisi Eddy”

“Naombeni nikazungumze naye””

“Sawa, mpeleke daktari alipo raisi”

“Sawa”

Dokta Wiliam akapelekwa hadi katika chumba alipo Rahab. Mlango ukagongwa na Rahab akafungua kimlango kidogo cha mlango huo wa chumba na kuchungulia nje.

“Dokta”

Rahab aliita kwa sauti ya upole huku machozi yakimlenga lenga usoni mwake.

“Naombeni mutupishe nizungumze naye”

Dokta Wiliam aliawambia wanajeshi hao na wakatii wakasimama umbali ambao sio rahisi kwa wao kuweza kuyasikia mazungumzo hayo.

“Unajisikiaje Rahab?”

“Najisikia faraja moyoni mwangu dokta”

“Kweli Rahab?”

“Ndio na leo ninahitaji niweze kuonana na Eddy”

“Eddy…..!!”

“Ndio nahitaji kuonana naye kuna mambo mengi sana ninahitaji kuzungumza naye”

Maneno ya Rahab yakamfanya dokta William kushusha pumzi nyingi sana kwania likuwa amekusudia kutengeneza dawa ambayo inaweza kuondosha maisha ya Rahab na asiweze kuonekana kabisa katika maisha haya ya sasa hivi”

“Amekubali kuja?”

“Ndio amekubali kuja kuonana nami, ila dokta ninaombi moja”

“Ombi gani?”

“Naomba kama inawezekana nitengenezee dawa yoyote ambayo inaweza kufupisha maisha yangu na nisionekane tena duniani”

“Rahab…..”

“Yaa sina faida yoyote kwenye hii nchi. Muda wangu wa kwenda kule alipo elekea mume wangu umefika, tafadhali dokta nakuomba uweze kunisaidia katika hili nahitaji kupumzika hivi sasa”

Dokta Wiliam akaka kimya japo hapo awali alikusudia kutengeneza dawa hiyo kisiri siri pasipo mtu yoyote kuweza kufahamu chochote.

“Una uhakika na maamuzi yako Rahab?”

“Ndio nina uhakika tafadhali ninakuomba uweze kuitengeza hiyo dawa, na nitakuomba uweze kumpatia Eddy pindi atakapo kuja hapa kunitembelea”

“Sawa”

Baada ya makubaliano hayo dokta William akamuita mwanajeshi aliye mleta eneo hilo na wakaeleka katika maabara ya hospitalini hapo na akaanza kutengeneza dawa hiyo huko moyoni mwake akiwa na maumivu makali kwani anakwenda kumuua kijana wake anaye mpenda sana.

***

“Najua utakuwa una huzuni mpenzi wangu, ila nafanya hivi kumfurahisha mam yangu”

“Usijali Adrus nimekuelewa, nimekubali uoe mwanamke mwengine. Yote ni kwa sababu ninakupenda na sihiaji kukupoteza”

“Nashukuru sana mke wangu nafurahi kusiki hilo. Na jambo jengine nimepata nafasi ya kuwa mlinzi wa karibu kabisa wa raisi Eddy Godwin hivyo basi nitaifanya kazi hiyo hadi pale atakapo toka madarakani”

“Sawa mpenzi wangu na mimi naomba unifanyie kitu kimoja”

“Kitu gani?”

“Naomba nipate uraisi wa nchi hii ya Tanzania sihitaji kurudi tena nchini Marekani”

“Usijali hilo mke wangu utaupata uraia”

“Asante”

Naomi na Adrus awakaendele kukaa hotelini hapo huku wakiburudishana kwa kuepea mapenzi mototo. Majira ya jioni Adrus akarudi ikulu kuendelea na majukumu yake kama ilivyo muahidi raisi Eddy Godwin. Akafika ikulu na kumkuta Eddy akiwa anajianda kwa safari hiyo.

“Nimechelewa muheshimiwa?”

“Hapana naujua ulihitaji kumpatia utamu bibie”

Eddy alizungumza kwa utani na kumfanya Adrus kutabasamu. Maandalizi ya raisi Eddy kuelekea mkoni Morogoro yalipo kamilika, akaingia kwenye helicopter ya ikulu pamoja na walinzi wake, huku helicopter nyingine mbili za jeshi zikiwafwata kwa nyuma. Safari yao haikuchukua muda mrefu wakafika katika kambi ya jeshi ambapo maandalizi ya kumpokea raisi Eddy Godwin yalisha fanyika.

Eddy akashuka kwenye helicopter na walinzi wake na kuelekea katika ofisi za kambi hiyo ya jeshi na kupokea ripoti nzima ya jinsi gani maiti za wanajeshi walio uwawa na Rahab.

“Kila familia ya mtu aliye ondokea na kijana wake, wapatiwe kiasi cha shilingi milioni mia moja kila famili”

“Sawa muheshimiwa raisi”

“Na video zote ambazo zilikuwa zinaonyesha juu ya mauaji na matukio yaliyo fanywa, hakikisheni kwamba muna ziweka sehemu za siri ambayo hakuna mtu wa aina yoyote ambaye anaweza kuziona au kuzipata kirahisi umenielewa mzee”

“Nimekuelewa muheshimiwa”

“Sasa nahiaji kwenda kuonana na Rahab”

“Ila muheshimiwa kuna maagizo ambayo yametoka kwa doktwa William anahitaji kuzungumza nawe”

“Yupo wapi?”

“Kwenye wodi ya wagonjwa”

“Sawa”

Raisi Eddy akaongozana na Adrus hadi katika wodi aliyolazwa dokta Wiliam, Adrus akataka kubaki nje ya wodi hiyo ila Eddy akamuomba waingia kwa pamoja, wakasalimina na dokta William,

“Nashukuru muheshimiwa kwa kuweza kufika”

“Usijali ni jukumu langu:

Taratibu dokta William akatoa sindani aliyo kuwa amificha kwenye mfuko wa suruali yake. Akamkabidhi Eddy mkononi mwake.

“Hii ni sindano ambayo ina sumu kali ambayo inaweza kumuua Rahab. Namini kwamba umesoma kitabu kile chenye siri hizo.”

“Ndio nimekisoma”

“Leo ndio muda sahihi wa kuweza kumuua, hata yeye mwenyewe anahitaji kupumzika.”

“Nashukuru kwa msaada wako dokta kwa maana hata mimi nilikuwa nimesoma zile mbinu ila nilishindwa kujua ni wapi nitaanzia kumdhuru Rahab”

“Ni kweli”

Raisi Eddy Godwin akamaliza kuzungumza na dokta William na wakatoka katika chumba hicho, moja kwa moja wakaelekea katika chumba alipo fungiwa Rahab.

“Naombeni muniache peke yangu”

Eddy alizungumza huku akimtazama Adrus usoni mwake. Adrus akatingisha kichwa cha kukubaliana na ombi hilo la raisi, wakaondoka aneo hilo pamoja na walinzi wengine. Eddy akagonga mlango huo taratibu Rahab akafungua kijimlango kidogo alipo muona ni Eddy akatabasamu sana. Taratibu Eddy akafungua mlango huo na kuingia ndani ya chumba hicho. Kwa haraka Rahab akamkumbatia huku akilia.

“Eddy najua kwamba umekuja kuniua, sinto kwenda kukuona tena kwenye maisha yangu. Naomba unipe penzi lako la mwisho Eddy tafadhali nakuomba mpenzi wangu”

Maeno ya Rahab yakamfanye Eddy kuanza kulengwa lengwa na machozi, kwani kuna mambo mengi sana mazuri wameyafanya na Rahab. Taratibu Rahab akaanza kuvua nguo zake na kubaki kama alivyo zaliwa. Eddy naye hakuona hiyana ya kuenenda kinyumbe na Rahab, akavua nguo zake kisha akamnyanyua Rahab na wakaanza kunyonyana midomo yao huku wakimwagikwa na machozi. Taratibu wakaanza kupeana penzi mototo, huku kila mmoja akiwa na uchungu sana moyoni mwake kwani ili kumsaidi Rahab na watu wengine waishi kwa amani ni lazima amuua jambo ambalo ni maamuzi magumu sana kwa Eddy. Hadi wanamaliza mzunguko wa kwanza kila mtu bado machozi yanamwagika usoni mwake.

“Rahab siwezi kufanya hilo unalo lihitaji kulifanya, siwezi kukuua. Sihitaji niishi kwa kukosa amani maisha yangu yote tafadhali nakuomba uchague hata maamuzi mengine”

Eddy alizugumza huku machozi yakiwa yamemwagika usoni mwake.

“Eddy siwezi kuendelea kuishi tena, hapa nipo na wewe tu ila ninajitahidi kuizuia hasira yangu kwako, la sivyo ninaweza kukudhuru na kukuua. Tafadhali kama una dawa uliyo pewa na dokta William tafadhali nakuomba unichome na nife na hii ndio itakuwa sababu ya pekee ya wewe kuendelea kuongoza nchi kwa usalama kwa maana utawaeleza wananchi kwamba nimekufa na watashuhudia mwili wangu na mazishi yangu na hakuna ambaye atakuuliza juu yauwepo wangu”

“Rahab”

“Najua Eddy ni maamuzi magumu kwako, ila tafadhali ninakuomba uweze kunichoma hiyo sindano”

“Rahab siwezi”

“Eddy ni wangapi umewau, ni wangapi umewaangamiza. Tafadhali fanya kwa ajili ya nchi na kizazi kijacho tafadhali mpenzi wangu”

Rahab alizungumza huku akimshika Eddy mikono yake.

“Tafadhali niue”

Eddy akavuta koti la suti yake, akatoa sindano aliyo kabidhiwa na dokta Willima, akafungua kifuniko cha sindano hiyo iliyo jaa dawa. Taratibu Rahab akaiweka shingo yake tayari kwa kuchomwa sindano hiyo, Eddy akajikuta akiweka sindano hiyo pembeni huku mwili ukiendelea kumtetemeka.

“Nichome”

“Nahitaji penzi lako”

“Eddy”

“Nahitaji penzi lako mpenzi wangu”

Rahab akamtazama Eddy kwa macho makali yalitisha Eddy na kujikuta akiigandamiza sindano hiyo kwenye shingo ya Rahab na kuisukuma dawa hiyo kwa nguvu, jambo lililo mfanya Rahaba kuanza kukakaama mwili wake. Hazikupita hata dakika mbili mwili wa Rahab ukakamaa kabisa mithili ya mti mkavu. Eddy akaanza kuangua kilio kizito sana na kuwafanya Adrus na watu wake kukimbili katika eneo hilo. Adrus akawazuia walinzi wengine kuingia ndani ya chumba hicho zaidi yake yeye. Alipo mkuta Eddy akiwa uchi kama alivyo zaliwa, taratibu akaufunika mwili wa raisi Rahab kwa koti la suti yake aliyo ivaa. Adrus hakuzungumza chochote zaidi ya kutoka ndani ya chumba hicho na kumuacha Eddy aendelee kuomboleza msiba huo wa mpenzi wake.

***

Baada ya mwenzi moja ya mazishi ya raisi Rahab, Adrus akaanza akawaoa Cookie na Naomi kwa harusi kubwa iliyo dhamini na raisi Eddy Godwin ambaye katika kipindi kichache tu cha kukaa madarakani watu walisha anaza kuona ndoto njema kwani, miradhi mingi ya kiserikali ambayo hapo awali haikuendelezwa na kupelekea kufa kabisa, akaifufua na kuipa nguvu kubwa na kusababisha wananchi wake wengi sana kupata ajira na uchumi wa nchi na raisi kwa ujumla ukaanza kupanda.

“Adrus”

Eddy alimuita Adrus wakiwa ofisini kwake.

“Ndio muheshimiwa”

“Najua wake zako kwa sasa ni wajawazito, japo hukupenda kuniweka wazi si ndio?”

“Ndio muheshimiwa nisamehe kwa hilo”

“Hapana wala usijali. Kuna swala ninahitaji unishauri”

“Swala gani?”

“Nimebakisha mwaka mmoja na nusu kabla ya uchaguzi mkuu, nahitaji kuachana na swala la uraisi na ninataka kuondoka Tanzania kabisa na kuhamia katika visiwa vyoyote mimi na familia yangu. Hata wewe ikihiaji unaweza kufwatana nami je unaonaje hili?”

“Mmmm muheshimiwa hilo ni swala zito kidogo, ukilinganisha kwamba wananchi wanakupenda sana”

“Yaa natambua hilo ila toka afe Rahab naongoza hii hiyo basi tu nifanyaje ila nafasi yangu ya pekee ni kuachana na hili swala la uongozi nahitaji kutengeneza mapenzi mazuri kwa wanangu kwani hiyo ndio famili yangu iliyo salia hapa duniani. Baba, mama, dada Manka wote walikuwa kwa miparangano ya visa vya kijinga tu”

Eddy alizungumza kwa sauti ya upole sana huku akitazama eneo la nje ya ikulu kupitia dirishani.

“Hayo ni maamuzi yako muheshimiwa”

“Sawa”

Usiku wa siku hiyo, Eddy akashauriana na Phidaya juu ya wazo la kuachia madaraka, japo kwa Phidaya ilikuwa ni jambo gumu kidogo kulielewa, ila mwishowe akakubali kuhusianana jambo hilo. Siku, wiki na miezi ikakatika hadi ikafika kipindi cha Eddy kukaa madarakani. Kama alivyo ahidi mwaka mmoja na nusu ulio pita, akatangaza mbele ya wananchi wote wa Tanzania kwamba hato gombania uraisi katika uchaguzi mkuu ujao. Haikuwa habari nzuri kwa wananchi wengi ambao wanampenda, ila kwa K2 na kaka yake ambao tayari kwa kutumia pesa zao walisha muweka Livna mikononi mwao kutokana na kiasi cha pesa kikubwa walicho weza kumpatia.

“Ni wakati wetu sasa kuchukua madaraka”

K2 alizungumza huku akitazama habari hiyo kwenye tv ya taifa.

“Yaa nilazima niwe mimi raisi ajaye na nina imani wananchi watanipa kura za kutosha”

“Ni kweli na ni wakati wetu wa kuwajibika kisiasa sasa”

Eddy mara baada ya kumaliza kuzungumza na wanahabari akarudi ofisini kwake na kuikuta familia yake yote ikimsubiria akiwemo Shamsa na mwanaye pamoja na Phidaya na mwanaye pasipo kumsahau Sa Yoo.

“Umefanya jambo la muhimu mume wangu”

Phidaya alizungumza huku akimkumbatia Phidaya.

“Kweli mke wangu. Ninawapenda sana wote na ni wakati wa kuondoka nchi Tanzania sasa, mara tu baada ya kuikabidhi nchi kwa raisi ajaye”

Mlango wa ofisi hiyo ukagongwa na Eddy akaruhusu mtu anaye gonga kuingia ndani ya ofisi hiyo. Adrus akaingia akiwa na Cookie pamoja na Naomi huku kila mmoja akiwa na mtoto wake na wote wamejaliwa kupata watoto wa kike wazuri kama mama zao.

“Na sisi pia tunajumuika nawe muheshimiwa kuondoka”

“Kweli?”

Sa Yoo aliuliza huku akiwa amejawa na furaha.

“Ndio”

“Na mama pia anaondoka nasi?”

“Ndio na mimi pia ninakwenda”

Akaingia mama Adrus huku akiwa ametabasamu sana. Kwa pamoja wakajikuta wakikumbatiana kwa furaha kwa manaa wamekuwa ni familia moja. Huku Eddy akizidi kujawa na amani kwani Anjelina na kijana wa Livna aliwaachia huru mwaka mmoja ulipo pita pasipo kuwadhuru na hakuona haja ya kutengeneza uadui mwingi ikiwa anahitaji amani ya moyo wake pamoja na familia yake na watu wote wanao mzunguka kwenye maisha yake.


MWISHOOOOOOO

 

0 comments:

Post a Comment

BLOG