Search This Blog

Wednesday, November 18, 2020

POWER SEHEMU YA 3/10

 

 


 POWER

WRITER…………………………………………EDDAZARIA G.MSULWA
WEBSITE………………………………………… www.storyzaeddytz.com
CONTACT……………………………………….. 0657072588/0768516188
AGE……………..18+ 

SEHEMU YA 3 KATI YA 10

 


Nikatabasamu kisha nikasimama wima. Tukapewa ishara ya kuanza kuingia uwanjani. Taratibu tukaanza kutembea hadi uwanjani, uwanja huu una mashabiki wengi sana ambao wengi wao wameshika wabango yanayo nikaribisha tena uwanjani. Tukajipanga mstari mmoja ulio nyooka huku Camila Alexander Diazi akiwa amesima mbele yangu. Ukapigwa wimbo wa taifa wa timu ya Spain kisha ukapigwa wimbow a taifa wa nchi hii ya Ujerumani. Tukabadilsiahana bendera na kapteni wa timu ya wapinzani. Leo hii timu yangu inaanza katika goli Kaskazini mwa uwanja huu. Kila timu ikazunguka nusu duara katikati ya uwanja huu na tukapewa dakika moja ya ukimya kwa kuwakumbuka waalimu wa shule ya Camila walio chinjwa na kundi la kigaidi huko barania Afrika liitwalo Al-Shabab.

Dakika moja ilipo kwisha, filimbi ikapigwa na refarii, kisha wachezaji tukatawanyika, kila mtu akasimama katika nafasi yake. Wapinzani wezetu wakaanzisha mpira huu, huku wakionekana kuumiliki sana mpira huu. Hatukuchoka katika kuutafuta mpira ambao wapinzani watu wana umiliki kwa kupigiana pasi zinazo fika kwa kila anaye kusudiwa kupewa mpria.

Wapinzani wetu wakafanya shambulizi moja kali sana, ila Frenando akafanikiwa kuunyaka mpira huo. Frenando akaupiga mpira mbele. Lukas akautuliza vizuri kifuani mwake kishaa kauweka chini, akanitazama nilipo na kupiga pasi ndefu iliyo anza kuambaa ambaa hewani, nikaanza kukimbia kuelekea kwa wapinzani wangu, huku kila mara nikiutazama mpira huu. Wachezaj wawili ninao kimbizana nao hawakusita katika kuutazama mpira huo. Kitendo cha mpira kutufikia tulipo, nikauunganisha kwa shuti kali ambao liliambaa hewani kwa sekunde kadhaa na kugonga mwamba wa juu wa wapinzani, kisha mpira ukatoka nje. Uwanja mzima ulisimama na kushangilia kwani kama mpira huo ungeingia golini basi lingekuwa ni goli moja la kihistoria katika machuano haya.

Inadi ya wachezaji wanao nikaba kwa timu pinzani ikaongezeka, wakaanza kunikaba wachezaji wanne wanne jambo lililo nifanya nianze kuuona mchezo mgumu kwa upande wangu, kwani kila mpira ambao ninaletewa na wachezaji wezangu, siumiliki hata kwa sekunde nyingi wanakuwa wananipokonya. Kipindi cha kwanza kikaisha pasipo kufungana

“Pole mume wangu”

Camila alizungumza huku akitembea pembeni yangu.

“Ndio mpira mpenzi wangu”

Nilizungumza huku tukiingia ndani ya chumba chetu. Kila mchezaji uso wake umetawaliwa na kuchoka, kwani mtandange huu ni wa kukata na shoka, yaani ni bora hata na mechi ya kwanza tulo cheza kwani tulifungwa na tulikuwa na hamasa ya kutafuta goli, ila mechi hii, karibia wachezaji wa timu pinzani wanakaba na wanaonekana hawana hata hamu ya kutafuta goli na itakuwa ni furaha yao wakiona tunagawana pointi.



“Mumecheza vizuri. Ila wapinzani wetu hawajaweza kutupa nafasi ya kufunga. Munachotakiwa kufanya hivi sana ni kuhakikisha kwamba viungo wa katikati munapanda na nyinyi wafungaji, wakipanda viungo kwenda kushambulia nyinyi munarudi kuwa viongo”

Kocha alizungumza huku akitutazama.

“Ndio mfumo gani tena huo kocha?”

Mchezaji mmoja aliuliza huku akimtazama kocha usoni mwake.

“Ni ZigZag. Wapinzani wote macho yao yapo kwa Ethan na Pinto. Wanawafanya wanashindwa kumiliki mpira. Mawinga wa pembeni, hakikisheni sasa hivi nyinyi ndio munakuwa munaongoza jaramba za kufunga. Safu ya mabeki, nanyi hakikisheni kwamba hapiti mshambiliaji yoyote wa upinzani. Mumenielewa?”

“Tumekupata kocha”

Baada ya kumaliza kutibiwa majeraha madogo madogo yakiwemo kubwanwa na misuli, tukaanza kurudi uwanjani.

“Mume wangu leo umeshikika”

Camila alizungumza kwa sauti ya chini huku tukitembea kwa pamoja.

“Yaani wee acha tu, wanakaba kama nyuki. Tena mtazame yule mchezaji namba sita uwanjani. Yaani kama nimepokonya mwanamke. Yaani nikigusa mpira tu huyu hapa miguuni”

“Hahaaaa acha hizo mume wangu. Nenda kanifungie goli bwana nifurahie”

“Sawa mke wangu”

“Nitakunyima na leo pia”

Maneno ya Camila yakanifanya nitabasamu tu huku nikiingia uwanjani na yeye akielekea kwenye eneo la benchi la ufundi. Wachezaji wote tukakamilika uwanjani, refaa akaanzisha mpira, huku wachezaji wa timu zote mbili tukionyesha haya ya kuhitaji kufunga goli. Kama vile kocha alivyo tuelekeza ndivyo tulivyo anza kucheza na kuwachanganya wapinzani wetu ambao muda wote macho yao yalikuwa kwangu na Pinto. Kazi yetu ikawa ni kuwakusanya upande mmoja wapinzani wetu, kisha mipira tunawapasia Alex na Lukas.

Ndani ya dakika kumi na tano za kwanza tukafanikiwa kupata goli la kuongoza ambalo amelifunga Lukasa, kwa kuunganisha pasi nzuri aliyo pewa na Rodguize kiungo wetu wa katikati. Furaha ikatawala uwanja mzima huku kila mtu akiwa amejawa na furaha kubwa sana.

“Wamachanganyikiwa, ni mwendo wa kuongeza kasi ya mashambulizi”

Niliwaambiwa wachezaji wezangu, huku tukiwa tumekusanyika duara moja, muda wa kushangilia. Tukatawanyika na mpira ukaanza tena, wapinzani wetu wakaanza kuelewa mfumo wetu, wakapunguza mazoea ya kutukaba mimi na Pinto na walicho kifanya ni kunza kujigawa mmoja mmoja kwa kila mchezaji wa timu yetu.

“Kampeni mchezo umebadilika tunafanyaje?”

Alex aliniuliza huku tukisubiria beki wetu apige mpira mbele.

“Turudini kwenye mfumo watu wa kawaida”

“Utasaidia?”

“Hatuna jinsi, hakikisha munalinda goli”

“Sawa”

Maagizo niliyo yatoa yakaanza kumfikia mchezaji mmoja baada ya mwengine, nikafanikiwa kupata mpira, nikautuliza chini, mchezaji ambaye leo amenikamia kuhakikisha sing’ari uwanjani, akanifwata kwa kasi, nikamtazama kwa macho yakumkazia, akajaribu kunyosha mguu ili kuuchukua mpira, nikauvuta mpira kwa nyum kidogo na kuufanya mguu wake upoteze muelekeo, nikaupitosha mpira katikati ya miguu yake, japo alijaribu kuibana ila akashindwa. Akajaribu kunipiga kikumbo nisimpite, ila nikamkwepa kisha nikaanza kukimbia na mpira pembezoni mwa chaki nyepe. Wakaongezeka na kuwa wachezaji wa nne huku wote wanaonekana kujawa na uchu wa kunipokonya mpira.

Nikaubana mpira katikati ya miguu yangu, nikaurusha juu kidogo na ukampita beki mmoja, nikauwahi kabla ya mchezaji mwengine kuuchukua, naye nikamfanya kama mwenzie. Nikatika kama ninaupiga mpura, ila nikausogeza kidogo pembeni na kumfanya beki mmoja kupitiliza huku akiserereka kana kwamba ameanguka na pikipiki. Nikaanza kuichezesha miguu yangu huku nikimtazama beki aliye salia, nikaukanyaga mpira na mguu wangu mmoja kisha nikazunguka nao na nikampita beki huyu akiwa amesimama pasipo hata kuthubutu kunyoosha mkono wake. Uwanja mzima ukafurika kwa shangwe, nikalitazama goli na kumuna kipa akiwa amesimama upande huu ninao tokea. Nikausogeza mpira kwa mbele kidogo kisha nikaachia shuti moja kali sana na kuufanya mpira uzunguke zunguke hewani, na ukaingia katika kona ya juu ya goli, japo kipa alijaribu kwa kadri awezavyo kuruka ili autoe ila akashindwa kabisa. Shangwe zikafumuka uwanja msimza. Nikaanza kukimbia kuelekea katika benchi la ufundi huku nikimyooshea Camila kidole. Nilipo mkaribia Camila akanikumabia kwa furaha huku kocha na wachezaji wengine wote nao wakinikumbatia.

“Kwa ajili yako mke wangu”

Nilizungumza kwa sauti huku nikiendelea kukumbatiwa. Camila akashindwa hata kuzungumza kitu na kubaki akimwagikwa na machozi tu.

Tukarudi unawanjani huku jina langu likiibwa na mashabiki wote. Mpira ukaanza tena huku wapinzani wetu wakiwa wamechanganyikiwa kabisa, kwani goli nililo lifunga hakika limeingia kwenye rekodi ya magoli bora katika michuano hii.

Hadi tunafika dakika ya mwisho, goli ni mbili bila. Tukaanza kuepeana mikono na wapinzai wetu, japo tumewafunga ila kwenye kundi letu wao ndio wanatufwatiwa nyuma tetu. Tukawaaga mashabiki wetu huku waandishi wa habari wakiwa makini katika kuniwinda ili kunihoji maswali mawili matatu. Nikaitwa na waandishi wa habari wawili na nikasimama katika eneo maalumu ya kuhojiwa huku nikiwa na Frendando.

“Kwanza hongereni sana kwa ushindi huu mzuri”

“Tunashukuru sana”

“Ethan unajisikiaje kufunga goli moja zuri sana ambali hakika hadi sasa hivi sijapata la kufananisha nalo?”

“Ahaa….ni furaha kwa kweli, unajua wapinzani wetu ni wazuri sana. Kipindi cha pili hawakunipa nafasi ya kufunga basi kipindi cha pili nikaapiza kufanya kila liwezekanalo kuhakikisha kwamba ninafunga na kweli nimefunga. Ninamshukuru sana Mungu kwa hilo”

“Hongera sana hii ni zawadi ya goli bora kwa mechi ya leo”

Muandishi huyu alinipa kiboksi ambacho ndani kina kiatu kidogo cha dhahabu.

“Nashukuru sana”

“Frenando Alemedo, hongera sana kwa kuto ruhusu goli kuingia nyavuni kwako”

“Nashukuru”

“Nini siri yako ya kunyaka kila mkwaju ambao walikuwa wakiutuma wapinzani wako na isitoshe ndio umerudi kutoka kwenye majareha?”

“Kila kitu ni kijituma na mazoezi, nilijitahidi kuhakikisha kwamba ninakuwa kipa bora na basi nitakuwa kipa bora kwenye hii michuano”

“Hongera sana na wewe umepata zawadi yako ya mchezaji bora wa mechi kutoka SuperSport”

“Tunashukuru”

“Hata tutwatakie siku njema”

“Asanteni”

Tukaondoka katika eneo hili na nikamkuta Camila akinisubiria, akanipoke zawadi yangu niliyo pesa kisha akanipiga busu la mdomoni na kuwafanya wa wapiga picha kila mmoja kujitahidi kupiga picha kadri ya uwezo wake. Tukarudi katika vyumba vya kubadilishia nguo. Kila mmchezaji hakusita kunipongea kwa juhudi niliyo ionyesha.

“Unajua nini Ethan”

“Mmmm….”

Muna ule yule beki alivyo kwua akiserereka, nilifumba macho kwa kweki, kwa maana ile miguu laiti kama ingekupata basi sasa hivi tungekuwa tunazungumza mambo mengine kwa kweli”

“Yaa na nilijua tu kwamba akili zake zitaishia pale, unajua ameserereka hadi ameacha alama uwanjani, kang’oa kabisa nyasi”

“Hahaaaaa…..”

Furaha ikazidi kutawala ndani ya chumba chetu hichi. Tukavaa track suit zeu kisha tukaelekea eneo lilipo basi letu tukapanda na kuanza safari ya kurudi kambini.

“Mume wangu ona ona”

Camil alizungumza huku akionionyesha jinsi goli langu linavyo rudiwa kurushwa kwenye kituo cha SuperSport 3. Nikaendelea kujitazama kwenye simu hii ya Camila, hakika kitu nilicho kifanya kwa mabeki hawa kitaandika histori kubwa sana kwenye maisha yangu.

“Wanalifananisha goli langu na Ronaldinho yule wa Braziel”

Nilizungumza huku nikimuonyesha kocha matangazo haya ya moja kwamoja tunayo yatazama kupitia simu ya Camila.

“Duu, na wanasema kwamba ni zaidi ya goli lake”

Nilizungumza kwa furaha.

“Ni historia umeandika, sasa usivimbe kichwa. Hakikisha kwamba unazidi kuishangaza dunia kwa mambo mengine mengi sana. Sawa”

“Sawa kocha”

Tukafanikiwa kufika hotelini salama salmin. Tukaingia kwenye vyumba vyetu. Mimi na Camila tukaanza kuoga kwa pamoja. Kutokana na hisia kali zilizopo kati yetu, tukashindwa kujizuia hisia zetu na kujikuta tukizama kwenye mahaba mazito ambayo kila mmoja alijitahidi kuhakikisha kwamba ana mridhisha mwenzake kwa kiwango cha juu. Tukamaliza mzunguko huu na tukajilza kwenye sinki hili la kuogea.

“Baby”

“Mmmmm”

“Una mpango gani na maisha yako ya mpira ya baadae?”

“Nitainia kwenye timu yoyote kubwa ambayo itanihitaji”

“Kama?”

“Liverpool, Real Madrid”

“Unaipenda sana Liverpool?”

“Yaa nina ipenda, ila kama watanihitaji kwa dau kubwa basi nitakubali kuungana nao?”

“Inabidi unifanye niwe wakala wako”

“Haahaaa”

“Ndio mume wangu, kila kitu kiwe kwa ajili ya familia yetu. Lazima nikusimamie kwenye kila jambo zuri ambalo badae litatufanya tuishi maisha mazuri”

“Usijali mke wangu, nina imani kwamba kuna mawakala wengi watajitokeza. Mbaya sina msimamizi, baba alisha fariki na aliniacha katika wakati mgumu kiasi wa kusimamia kampuni zake. Kwa hiyo nahitaji mtu makini katika maisha yangu ya soka”

“Sawa mume wangu, kama utapenda utaniweka mimi?”

“Nitalifikiria hilo, il aje siku ukiwa mjamzito kweli utaweza kusafiria masafa ya mbali kuingia mikataba na timu kubwa kubwa?”

“Kwani mume wangu mimba nina ibeba mwaka mzima. Tutapanga mpango madhubuti na tena mume wangu, tufanye jambo juu ya hili sawa. Maliza masomo yako nami nimalize yangu kisha tutaendelea na biashara yetu ya mpira huu wa miguu”

“Sawa tuombe Mungu”

“Timu ambayo itataka kukunununua, ni lazima ikulipe paund dola laki tano mshabara wa wiki”

“Mmmm mke wangu, unataka nikawe mbuzi wa albadili huko kwenye timu za watu?”

“Kwa nini?”

“Msaada wangu kwenye timu ni lazima uwe mkubwa kutokana kile wanacho nilipa”

“Mungu atakujalia Mume wangu”

“Kweli na utafanikiwa tu mume wangu”

“Haya”

Tukamaliza kuoga, tuvaa nguo za kushindia kwa usiku huu. Tukajumuika na wachezaji wezangu katika kupata chakula cha usiku. Tukiwa katika eneo hili tukaanza kuwaona walinzi wa baba Camila wakiingizana humu ndani jambo lililo tufanya watu wote humu kupatwa na mshangao. Tukawaona wazazi wa Camila ambao kwa kipindi hichi ni maarufu sana hapa Ujerumani, hii ni kutokana na nafasi ya kiti cha uraisi anacho kigombania baba yake.

Mimi na Camila tukanyanyuka na kuwakaribisha kwa furaha sana.

“Tumewafanyia suprize”

Baba Camila alizungumza huku akinisalimia kwa kunipa mkono.

“Tunashukuru sana, karibuni sana wazazi wetu”

“Asanteni”

Tukakaa nao katika meza tuliyo kuwa tumeketi.

“Kwa goli ambalo Ethan umefunga leo, yaani nilisime hapana. Nilazima nije nikuangalie vizuri mwanangu. Heee hapana kwa kweli”

Mama Camila alizungumza huku akiwa amejawa na furaha kubwa sana.

“Nashukuru sana mama. Kumbe mama na wewe huwa unatazama mpira ehee?”

“Yaani toka ulipo anaza kucheza wewe, nikaanza kupenda mpira. Unakumbuka ile siku ambayo Camila alitaka kujirusha gorofani?”

“Ndio ndio nakumbuka mama?”

“Sasa siku ile ndio nilipenda kutazama mpira, hakika nina mkwe ambaye anatufanya kila muda tujisikie amani katika mioyo yetu”

“Nashukuru sana mama”

“Kocha wenu yupo wapi?”

“Yule kule”

Nikamuita kocha kwa ishara, akasimama na kutufwata eneo hili tulio kaa.

“Hongera sana kwa wachezaji wako ulivyo waanda. Yaani wanatupa buruni moja nzuri sana”

“Nashukuru sana mkuu”

“Nikipata nafasi, nitapendekeza uinoe timu ya taifa na hii mashine yako hapa nayo iwepo katika timu yako ya Taifa”

Maneno ya baba Camila yakanistua kidoo, kwani katika maisha yangu yote ya kuishia hapa Ujerumani, sijawahi kufikiria kuichezea timu ya taifa ya nchi hii japo nina uraia wa hapa Ujerumani. Nchi yangu mimi ni Tanzania na mimi ni Mtanzania na kamwe sinto isaliti Tanzania hususani katika maswala ya mpira ninao cheza.



Nikatabasamu usoni mwangu, ili kuficha msimamo wangu nilio nao moyoni mwangu, amboa kuutangaza kwa sasa itanigarimu sana maisha yangu katika soka.

“Nitashukuru sana mkuu, nami nitajitahidi kuhakikisha kwamba ninaipelekea timu ya taifa katika viwango vya juu kabisa vya kimataifa vya Fifa”

“Nashukuru sana”

Kocha na baba Camila wakamaliza kusalimiana na kisha kocha akarudi kukaa katika kite chetu.

“Tunaweza kupata muda wa kuzungumza nanyi wawili?”

Mama Camil alizungumza huku akitutazama usoni mwetu.

“Ndio hakuna tatizo mama yangu”

“Basi twendeni tukazungumze”

Nilizungumza huku nikimtazama mama Camila usoni mwake. Tukaondoka eneo hili na kuingia kwenye moja ya ofisi iliyo andaliwa kwa ajili yetu. Tukaingia watu wa nne na walinzi wote wakabaki nje. Ukimya wa sekunde kadhaa ukatawala katika eneo hili huku mimi na Camila tukiwa tunawatazama.

“Nina imani kwamba mumebakisha mwaka mmoja kabla hamjafikisha kiwango cha miaka kumi na nane si ndio?”

“Ndio ndio baba”

Niliitika wa unyonge, kwani mazungumzo ambayo naamini yanazungumzwa hapa ni muhimu sana.

“Na munapenda sana?”

“Ndio mama”

“Labda nichukue muda mwengine Ethan, kwa niaba ya familia yangu, ninakuomba unisamehe sana kwa yale yaliyo jitokeza kati yako wewe na Camila pamoja na familia nzima. Hakika tulishindwa kumzuia mtoto wetu, akafanya jambo la kipumbavu ambalo hadi leo hii, linaniumiza sana”

“Musijali wazazi wangu, ninaelewa hilo na tulisha lizungumza, tuacha yaliyo pita tutazame haya taliyopo mbele yetu”

“Nafurahi kusikia hivyo”

“Mimi na baba yenu, niliona kuna umuhimu endapo mukifikisha miaka kumi na nane muvishane pete ya uchumba, kisha nyinyi mutapanga ni muda gani munaweza kuoana”

Jambo hili kidogo likatufanya tustuke kwani tangu tuanze mahusiano yetu hatukuwahi kuketi chini na wazazi hawa na kuzungumzia lolote kuhusiana mapenzi yetu.

“Sawa sisi hili halina tatizo wazazi wangu. Nipo tayari kumuoa Camila kwa garama ya aina yoyote mutakayo nitajia”

“Hapana, unayo yafanya kwenye maisha ya famili hii ni garama tosha. Nakukabidhi mwanangu. Kumbuka ni mtoto wetu wa pekee, hatuna mwengine hata wa kusingizia na wala hakujawahi kuwazia kama tutapata mwenzake.”

“Musijali, tambueni kwamba nafanya kila jambo kwa ajili ya Camila. Ninaandaa familia bora kwa ajili yake, ninawahakikishia kwamba mtoto wenu yupo katika mikono salama. Mikono ambayo hakuna ambaye ataweza kuichafua””

“Asante sana mwanangu Ethan. Kuna jambo jengine nilizungumza na baba yako hapa akalipitisha. Kama unavyo fahamu tupo kwenye kipindi cha uchaguzi. Kila anaye gombani kiti hichi anafanya analo weza kuhakikisha kwamba anapata nafasi ya kuwa raisi. Nikiwa kama kampeni meneja wa baba yenu, nilikuwa nina pendekeza Ethan uweze kufanya tangazo moja la kumsaidia baba yako ili katika uchaguzi huu aweze kushinda?”

“Hili halina tabu mama, nakumbuka Camila nilisha kuambia hili si kweli?”

“Yaa kweli uliniambia”

“Hilo halina tatizo, nyinyi andaeni tu tangazo na nitalifanya kwa moja mmoja”

“Tunashukuru sana”

“Endapo Mungu akinijalia kuingia ikulu, nitakurudishia kiasi ulicho wekeza japo si kwa siku moja basi hata taratibu taratibu kwa maana nina imani kwamba wewe ni mfanya biashara, umetoa kiasi hicho kwenye makampuni yako kuhakikisha kwamba mambo kwa upande wangu yanakwenda vizuri nami nitalipa fadhila kwa kuyapunguzia makampuni yako kodi”

“Nashukuru sana baba”

Nilizungumza huku nikiwa nimejawa na furaha kwani katika vitu ambavyo ninavichukia katika biashara nikulipa kodi kubwa serikalini.

“Kesho Ethan muna ratiba gani na kocha wako?”

Mama Camila aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.

“Kesho nahisi tutapumzika tukisubiria mzunguko wa mtaano”

“Sawa, basi kesho tutatuma walinzi waje wawachukue na wawalete studio uweze kutengeza tangazo la kempeni”

“Usijali mama yangu”

“Na mimi mama nahitaji kuwemo kwenye tangazo hilo”

“Sawa tutaangalia kama muandishi wa tangazo atakupatia nafasi basi nawe utakuwepo”

“Nashukuru mama”

Tukazungumza mazungomzo mengi sana na mipango yetu ya baadae kisha wazazi wa Camila wakaagana na wachezaji wa timu yetu kisha wakaondoka. Nikamueleza kocha juu ya ombi nililo ombwa la kwenda kutengeneza tangazo la kampeni, kocha hakuwa na kinyongo na jambo hilo zaidi alichi kihitaji niweze kuwa makini. Nilipo maliza kuzungumza na kocha nikaingia chumbani na kumkuta Camila akiwa amejilaza kitandani kama alivyo zaliwa. Nikamtazama kwa muda huku nikimmezea mate ya uchu, taratibu nikavua nguo zangu kisha nami nikapanda kitandani. Nikaanza kumpapasa mapajani mwake.

“Jamani Ethan tulale bwana”

“Nina hamu na wewe bwana mke wangu”

“Mmmmm…..”

Camila alinung’unika kwa sauti iliyo jaa mahaba. Kabla sijafanya kitu chochote, simu yangu ikaanza kuita, nikashuka kitandani na kuichukua juu ya meza. Nikaitazama namba hii ya mwanasheria wa kampuni zangu, kisha nikaipokea na kuiweka sikioni mwangu.

“Ndio mwanasheri?”

“Nina habari nzuri kidogo japo sio sana”

“Nimabie ni habari gani?”

“Vijana wamesha fika nchini Tanzania, na wapo kwenye hicho kijiji, na hivi sasa wapo kwenye hicho kijiji na wanafanya upelelezi wa kufahamu ni wapi alipo mama yako”

“Ohooo asante Mungu, naomba unifahamishe kila kitu kinacho endelea sawa”

“Sawa mkuu, kila kitu nitakujulisha hata kwa meseji”

“Nashukuru”

Nikakata simu huku moyo wangu, ukiwa ametawaliwa na furaha sana.

“Kuna nini mume wangu?”

“Wanakaribia kumpata mama yangu?”

“Kweli?”

“Ndio mke wangu”

Camila akanikumbatia kwa nguvu huku naye akionekana kujawa na furaha juu ya hili swala hili.

“Nina hamu ya kumuona mama yangu mkwe”

“Mungu ni mwema atasaidia kwa kweli”

Camila akanionyesha picha za mama zilizipo kwenye simu ambazo zinamuonyesha alivyo tekwa.

***

Asubuhi na mapema tukaingia katika helicopter maalumu iliyo agizwa kuja kutuchukua hapa hotelini. Tukaelekea katika mji wa FrankFurt ambapo ndipo ilipo kambi ya kampeni ya baba Camila. Tukapokelewa na mama Camila na moja kwa moja tukaelekea katika studio kubwa za televishon ambayo ni mali ya babu Camila aliye kuwa raisi kabla ya raisi wa hivi sasa ambaye naye muda wake unakwenda kuisha.

“Mke wangu nahisi kijimoyo kina nidunda dunda?”

Nilizungumza kwa sauti ya chini huku nikimnong’oneza Camila sikioni mwake.

“Usiogope mume wangu jiamini”

“Mmmmm, unajua sijawahi kufanya vitu kama hivi na jua kila mtu ana ujuzi sehemu yake”

“Haahaa, hembu vuta pumzi kwa nguvu kisha iachie taratibu”

Nikafanya kama Camil alivyo nieelekeza.

“Unajisikiaje?”

“Kidogo nafufuu”

“Ethan kunata na Gibson, huyu ndio muongozaji wa kutengeneza tangazo hili. Gibson nina imani sina haja ya kukutambulisha huyu ni mkwe wangu”

“Usijali madam, ninamtambua sana Ethan”

“Nashukuru, sas anaomba uweze kumpatia maelezo ya jinsi gani atakavyo weza kuanza kulicheza tangazo”

“Sawa”

“Jikaze mume wangu”

Camila aliniambia kwa kunikongoneza. Nikamjibu kwa kutingisha kichwa, tukaingia katika moja ya chumba ambacho kina wadada dada wengi pamoja na nguo nyingi za kubadilishia. Eneo hili la ukumbi ni kubwa sana na limegawanyishwa katika vyumba vyumba kadhaa. Gibson akanipatia kitabu kidogo. Wadada wote humu ndani, dhairi wanaonekana kuna na hamu hata ya kunigusa, ila kutokana tupo kazini hakuna aliye thubutu kunisogelea.

“Maelezo kwa ufupi yaliyomo ndani ya hicho kitabu, yanaelezea jinsi unavyo takiwa kuigiza ukiwa mtaani, unakimbia na mpira miguuni. Unalikuta hili kundi la wadada, unawauliza kwamba wanajua nani ni kiongozi mzuri wa kumchagua. Wadada hawa watakuwa wanashangaa shangaa, utavua begi lako mgongoni, utatoa bando la vipeperushi na kuwakabidhi mmoja baada ya mwengine na watakuwa wanakuzunguka huku wanakushika shika mwilini mwako. Hadi hapo umenielewa Ethan?”

“Ndio nimekuelewa, endelea”

“Utaachana na wadada hao na utaendelea kukimbia na mpira, mbele kidogo utakutaa na Camila akiwa anahangaika kuliweka sawa sawa tambaa kubwa lenye picha ya mgombea uraisi. Utakacho fanya wewe utarudi nyuma kidogo kisha utapiga suti kali, mpira utagonga katika sehemu ya tambara hilo iliyo jikunja kisha taratibu tambara hilo litafunguka na kuonyesha picha vizuri ya mgombe uraisi, mutalitazama kisha mutasema maneo ya kumchagua mgombea uraisi, sawa”

“Sawa”

“Hapo nywele zako zitatengenezwa kidogo na utafanyiwa makeup”

“Poa poa”

“Make anzeni kumshuhulikia Ethan, ninakwenda kumuelekeza Camila. Endelea kusoma taratibu ili uweze kuelewa, sawa?”

“Sawa”

Wadada waanne maalumu kwa shuhuli ya kunipodoa wakaanza kazi waliyo agizwa. Nikayarudia kuyasoma maeleo hayo na nikayaelewa vizuri. Baada ya muda kadhaa wakamaliza shuhuli hiyo. Tukatoka nje ya studio hizi na kuingia mtaani na kuanza kutengeneza tangazo hilo. Nikavaa jezi zangu za michezo pamoja na kibegi kidogo kisha nikaanza kuigiza zoezi hili. Hapo awali kidogo liliniwia ugumu kuigiza, ila kadri jinsi nilivyo igiza ndivyo jinsi nilivyo jikuta nina himli tamhazo hilo. Hadi inafikama majira ya jioni tukamaliza kutengeza tangazo hili na ambalo hakika ni zuri sana.

“Mume wangu kuna missed call thelathini kwenye simu yako”

Camil alizungumza huku akinikabidhi simu yangu

“Zimetokea wapi?

“Sijatazama, unaweza kutazama”

Nikafungua missed call hizo na kukuta zimetoka kwa mwanasheria wa kampuni. Nikampigia, simu yake haikuita snaa ikapokelewa.

“Mkuu ulikuwa wapi?”

Mwanasheria alizungunguza huku akiwa na wasiwasi mwingi sana.

“Ohoo samahani sana mzee nilikuwa nina fanya tangazo moja hivi”

“Sawa, nina habari kutoka nchini Tanzania”

“Ehee niambie”

“Mama yako amepatika”

“Kweli?”

Niliuliza kwa shauku iliyo ambatana na furaha kubwa sana.

“Ndio amepatika, ila…….”

Mwanasheria alizungumza kwa sauti ya upole na unyonge kidogo.

“Ila nini?”

Nilimuuliza mwanasheria huku furaha yangu ambayo nilikuwa nayo ikaanza kunipotea taratibu.

“Hali yake sio nzuri, katika harakati za kumkomboa kwa bahati mbaya alipunyuliwa na risasi ya kichwani mwake na kumfanya apoteze fahamu, na ninavyo zungumza hivi sasa, wapo njiana wanakuja naye nchini humu”

Nikajikuta nikinyon’gonyea na taratibu nikakaa chini na kumfanya Camila na watu wengine kunishangaa, kwa maana ni muda mchache tu wametoka kuniona nikiwa nimejawa na furaha sana



Camila akachuchumaa kwa haraka, akaichukua simu yangu mkononi mwangu na kuiweka sikioni.

“Ni Camila ni nini kinacho endelea?”

Camila aliuliza kwa shahuku kubwa sana, huku akinitazama usoni mwangu. Habari aliyo ipata hata yeye mwenyewe akaonekana kumnyong’onyeza. Muongozaji wa tangazo hili akatufwata sehemu tulipo.

“Vipi jamani kuna tatizo?”

Camila akaibi kwa kutingisha kichwa huku akimtazama muongozaji huyu wa filamu.

“Nahitaji kwenda uwanja wa ndege sasa hivi”

Nilizungumza huku nikimtazama Camila usoni mwake.

“Hakuna tatizo Ethan”

Muongozaji wa tangazo hili alizungumza, taratibu Camila akaninyanyua akisaidia na muongozaji huyu wa tangazo, nikaingizwa ndani ya gari, kisha baada ya muda kidogo Camila naye akaingia ndani ya gari na safari ya kuondoka eneo hili ikaanza huku tukiwa tumetanguliwa na gari la walinzi wa mama Camila. Furaha na amani vikanipote kabisa moyoni mwangu. Akilini mwangu, akili yangu inamuwaza tu mama yangu ambaye hali yake ni mbaya sana.

“Mume wangu usijali kila jambo litakwenda vizuri sawa?”

Nikajibu kwa kutingisha kichwa tu na safari ikaendelea. Ikatugarimu kama lisaa moja kufika katika kiwanja cha ndege. Nikamkuta mwanasheria akiwa katika eneo hili akimsubiri mama yangu kufikishwa hapa.

“Itagarimu masaa ngapi kufika hapa?”

“Kama masaa lisaa moja na dakika aroboini na tano hivi. Na nimesha andaa magadaktari bingwa. Akipokelewa ataingizwa kwenye helicopter ya hospitali na atawahishwa hospitalini”

“Nashukuru kwa kila jambo”

Nilizungumza kwa sauti ya unyonge sana. Masaa yakazidi kusonga mbele huku kila baada ya nusu saa mwana

sheria aliwasiliana na vijana tulio wapa kazi ya kwenda kumkomboa mama yangu.

“Wapo wapi?”

“Kama baada ya dakika kumi ndege ikatua hapa”

Mwanasheria alizungumza huku akitazama saa yake ya mkononi. Madaktari wapatao wanne wakakaa tayari kwa ajili ya kumpokea mama. Ndani ya dakika kumi alizo niambia mwana sheria, ndege maalumu ya kukodi taratibu ikatua kwenye uwanja huu. Wahudumu wa maalumu wa uwanja huu, wakaanza kukimbilia kwenye eneo ndege hiyo ilipo simama huku wakiwa wameongozana na madaktari wote wanne walio beba kitanda maalimu cha kukunjua. Sikuona haja ya mimi kuendelea kuhushudia mambo kwa mbali, nikaanza kukimbia kuelekea kule walipo. Nikafika na kukuta wakimtoa mama yangu ndani ya ndege hii, macho yakanitoka sana, kwani ni miaka mingi sana sijawahi kumuona mwana mama huyu. Kumbu kumbu kadhaa zikaanza kujirejea kichwani mwangu juu ya maisha yangu na huyu mwana mama, ila kila nilipo jaribu kuzikumbuka vizuri, nikashindwa kabisa.

“Kitanda hichi kikaanza kusukumwa hadi kwenye gari la wagonjwa, likafungwa kwa haraka na kuelekea katika uwanja mdogo wa helicopter.

“Mkuu kina helicopter ya kampuni, ipo hapa unaja wa ndege tayari kwa kuelekea hospitalini”

Mwanasheria alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.

“Sawa twende”

Tukaanza kukimbia kuelekea kwenye helicopter hiyo, huku Camila naye akiwa hayupo mbali nami. Tukaingia ndani ya helicopter hiyo na safari ya kuelekea hospiyalini ikaanza. Sikuzungumza kitu chochote hadi tukafika katika uwanja wa helicopter wa hospitali hii kubwa na nzuri. Tukashuka na kupokelewa na nesi mmoja na moja kwa moja tukaanza kupelekwa kwenye chumba cha upasuaji. Uzuri wa eneo hili la chumba cha upasuaji kuna kioo kikubwa ambacho mtu ukiwa nje ya chumba hichi unaweza kuona kinacho endelea ndani ya chumba. Tukawashuhudia madaktari jinsi wanavyo endelea na kuifanya kazi yao ya kuhakikisha kwamba wanayaokoa maisha ya mama yangu yanakuwa salama. Baada ya nusu saa mama Camia naye akafika katika eneo hili, kwa haraka akanikumbatia kwa nguvu huku akinipiga piga mgongoni mwangu taratibu. Machozi yakanimwagika na nikashindwa kujibu kitu chochote. Dada Mery naye akafika katika eneo hili, alipo tuona kidogo akaonekana kujawa na mshangao kwa maana toka nianzishe mchakato wa kumtafuta mama yangu, sikuwahi siku hata moja kumueleza dada Mery wala bibi Jane Klopp.

“Ethan ni kitu gani kinacho endelea?”

Dada Mery alizungumza huku akinisogelea karibu yangu. Akanitazama usoni mwangu kwa sura iliyo jaa wasiwasi mwingi.

“Ni mama”

“Mama yupi Ethan?”

“Mama yangu mzazi”

“Ohoo jamani?”

Dada Mery alizungumza kwa upole na unyonge mkubwa sana. Taratibu akanikumbatia huku akinibembeleza, Gafla tukawaona madaktari wakiwa katika harakati harakati nyingi ndani ya chumba hicho na wakanifanya niweze kukimbilia kwenye kioo hichi na kutazama ndani. Madaktari wengine wazee wakaingia ndani ya chumba hichi jambo lililo tufanya tujawe na wasiwasi mwingi sana.

Kitu kilicho zidi kutuchanganya ni mara baada ya mapazia ya kijani kufungwa kwenye vioo hivi na tukashindwa kuona kinacho endele ndani ya chumba hichi.

“Ni nini kinacho endelea?”

Niliuliza kwa sauti ya unyonge, hapakuwa na mtu aliye weza kunijibu. Camila akajikaza na kunikumbatia kwa nguvu.

“Nahitaji kuingia ndani humu”

“Ethan huwezi kufanya hivyo, kumbuka madaktari wapo kwenye kazi mume wangu”

“Nimesema ninataka kuingia”

Nilizungumza kw ukali sana huku nikimuachia Camila, kila mtu anaye nitazama akaonekana kunishangaa sana kwani maamuzi niliyo yafanya ni ya ukali sana. Nikafungua malango wa chumba hichi, manesi wawili wakaniwahi kwa haraka hata kabla sijapiga hatua yoyote.

“Tafadhali, tunakuomba uweze kutoka humu ndani Mr Ethan”

“Nahitaji kuzungumza na mama yangu”

Nilizungumza kwa sauti ya unyonge ila iliyo jaa msisitizo mkubwa sana.

“Jinsi unavyo endelea kupoteza muda kuwemo ndani ya hichi chumba ndivyo jinsi unavyo zidi kuiweka hali ya mgonjwa katika wakati mbaya zaidi. Tafadhali toka ndani ya chumba”

“Ni mama yangu”

“Ndio tunajua, ila acha tufanye kazi yetu Mr Ethan”

Mwanasheria akanishika mkono na taratibu akanitoa ndani ya chumba hichi.

“Nahitaji kuzungumza nawe”

Nilimuambia mwana sheria huku nikimtazama usoni mwake. Nikaanza kuondoka katika eneo hili pasipo kumuaga mtu yoyote. Tukafika katika kordo ya kuelekea katika eneo la chumba cha upasuaji.

“Ndio mkuu”

“Endapo mama yangu atakufa, nahitaji kumuua mtu mmoja baada ya mwengine walio husika katika hili jambo. Umenielewa?”

Nilizungumza kwa hasira huku nikimtazama mwana sheria usoni mwake.

“Sawa mkuu nimekuelewa”

“Ninaweza kuzungumza na vijana wako?”

“Si kwa muda huu muheshimiwa. Inabidi tuweze kukaa hapa tufahamu hali ya mama ina endeleeaje”

“Nalijua hilo, ila ninataka kuhakikisha kwamba nao wanapitia magumu kama magumu haya ambayo ninayapitia mimi kwa muda huu”

“Nimekuelewa muheshimiwa”

“Nitengenezee mfumo wa kuhakikisha kwamba ninamfahamu adui yangu mkuu na timu yake nzima aliyo shirikiana nayo”

“Sawa mkuu”

Nikarudi katika chumba cha kusubiria huduma, Camila akanisogelea karibu na sehemu niipo simama na akanishika kiuno changu.

“Kila kitu kinakwenda kuwa salama mume wangu sawa”

“Nashukuru”

Nilimjibu Camila kwa ufupi, akanibusu mdomoni mwangu na wala sikuweza kuwa na hisia za aina yoyote kwake. Baada ya masaa mawili na nusu mlango ukafunguliwa na akatoka daktari mkuu wa oparesheni hii. Watu wote tukasimama mbele yake huku tukimtazama usoi mwake.

“Poleni sana kwa kusubiria”

“Tunashukuru”

Mama Camila alijibu kwa kujiamini.

“Tunashukuru Mungu upasuaji umeenda vizuri, na tumefanikiwa kutoa damu iliyo kuwa imeganda kwenye ungong”

“Ohoo asante Mungu”

Mama Camila alijibu kwa unyenyekevu mkubwa sana.

“Sasa hivi tutamtoa mgonjwa humu na kumpeleka katika chumba cha wagonjwa mahututi. Humo atakaa kwa muda hadi pale hali yake itakapo kaa vizuri”

“Je anaweza kuzungumza?”

Nilimuuliza daktari huku nikimtazama usoni mwake.

“Hapana, kwa sasa hawezi kuzungumza, na kuna mambo kadhaa tutayazungumza ofisini, au kama nyote hapa ni wana familia basi ninaweza kuyazungumza sasa hivi?”

“Wewe zungumza tu dokta”

Nilitoa ruhusa hii kwa maana tuliopo hapa wote ni watu ambao ni msaada mkubwa sana kwangu.

“Kuna matatizo yamempata mama, nitayaeleza kwa hali ya kawaida tu na si kitaaamu sana.”

“Wewe zungumza tu daktari”

“Mama hato kuwana uwezo wa kukumbuka mambo yaliyo tokea na wala hato kuwa na uwezo wa kuona tena labda tu zitokee baraka za mwenyezi Mungu tu aweze kurudi katika hali ya kawaida”

Mwili mzimza ukazizima, nikahisi kunyong’onyea miguu yangu, mwana sheria akawahi kunishika kabla sijaanguka chini. Kitanda alicho lazwa mama kikatolewa humu ndani huku kitanda hichi kikiwa kimezungukwa na manesi sita.

Tukaongozana na manesi hawa hadi kwenye chumba kimoja kikubwa, wakatuomba tuwasubirie waandae chumba hicho vizuri kisha sisi nasi tuingie kumtazama. Baada ya dakika kama kumi na tano tukaruhusiwa kuingia ndani ya chumba. Nikaingai peke yangu ndani ya chumba hichi na kumkuta mama akiwa anapumulia amshine huku nesi mmoja akiwa amesimama pembeni ya kitanda hicho. Machozi yakazidi kunibubujika nikiwa ninamuangalia mama yangu, hali yake kwa kweli ni mbaya sana. Mwili wake ume dhohofika na anaonekana ni mwana mama amabt maisha yake yalikuwa ni mabaya huko alipo kuwaa kiishi.

“Mama”

Niliita kwa sauti ya unyonge kiasi huku nikijaribu kumshika mama mkono. Mama hakuweza hata kupepesa jicho lake, machozi yakaendelea kububujika usoni mwangu, nesi alipo ona hali yangu inazidi kuwa mbaya akaniomba niweze kutoka ndani ya chumba hichi. Sikuweza kubisha maamuzi ya nesi huyu, nikatoka ndani ya chumba hichi huku nikiwa nimejawa na dukuduku kubwa sana moyoni mwangu. Wakaiingia watu wengine nilio ambatana nao mmoja baada ya mwengine kumuona mgonjwa.

“Mungu atamsaidia mama atapona sawa mwanangu Ethan”

Mama Camila aliniambia mara baada ya kutoka katika chumba cha ICU.

“Sawa mama”

“Inabidi uende kula chakula sasa”

“Mama sijikii kula”

“Jitahidi tu mwanangu sawa”

“Sawa”

“Ethanm nitakwenda nyumbani na nitamueleza mama hili lililo jitokeza sawa mdogo wangu”

“Sawa dada”

“Hakikisha unapata chakula kama alivyo kueleza dada hapa”

“Poa poa”

Dada Mery akaniaga na kuondoka zake. Mwanasheria akaniita pembeni kwa ishara, nikamfwata.

“Vipi mkuu nikuandalie chumba katika hoteli ya hapa karibu?”

Nikaa kimya kwa muda huku nikifikiria cha kuzungumza.

“Nahitaji kukaa hapa”

“Sawa ngoja nikakutafutie chakula”

“Hapana, sihitaji chakula kwa sasa, nipo vizuri”

“Sawa mkuu basi naomba na mimi niweze kuelekea nyumba nikapumzike kidogo”

“Sawa wewe chukua muda wa kutosha pale nitakapo kuhitaji basi nitakufahamisha uweze kuja hapa”

“Sawa”

Mwanasheria na yeye akaondoka eneo hili na kuniacha nikiwa na Camila.

“Mume wangu naomba nikaongozane na walinzi nikachukue chakula kisha nirudi hapa, nitakuwa nawe na sinto kuacha peke yako sawa mume wangu”

“Sawa”

Camila akaninyonya midomo yangu kidogo kisha akaondoka katika eneo hili. Ethan mwenzangu akakaa pembeni yangu huku akinitazama usoni mwangu.

“Vipi mbona una huzuni sana?”

“Kwani hujui kilicho tokea Ethan?”

“Sikuhizi hunishirikishi mambo yako rafiki yangu, hadi pale utakapo kuwa na shida ndio una nikumbuka”

“Sio hivyo Ethan”

“Ila?”

“Kichwa changu hakikuwa vizuri kabisa”

“Sio hakikuwa vizuri rafiki yangu, kwa swala dogo kama hili kweli ulishindwa kunishirikisha mimi, hadi umeamua kutumia garama nyingi sana kwa vitu hivi?”

Ethan alizungumza kwa kulalamika.

“Samahani kwa hilo”

“Njoo nikuonyeshe kitu”

Ethan alizungumza huku akinyanyuka hapa pembeni yangu. Nikanyanyuka na tukaingia katika chumba cha alicho lazwa mama.

“Huyu ni nani yako?”

“Ethan aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.

“Ni mama yangu?”

“Unaikumbuka sura ya mama yako vizuri?”

Swali la Ethan likanifanya nikae kimya kwa muda huku nikimtazama mama huyu.

“Hapana”

“Kwa nini umeamini kwamba huyu ni mama yako?”

“Ethan, moyoni mwangu, ninahisi kabisa sura ya mama yangu”

“Acha ujinga Ethan, ni watu wangapi weusi ambao una fanana nao, unataka kusema kwamba ni ndugu zako. Hapa umechezewa mchezo wa ajabu. Sasa ni hivi huyu sio mama yako, mumepumbazwa na unapo pelekwa ni kufilisiwa kila kitu chako na utabambikiwa kesi ya mauaji umenielewa”

Maneno ya Ethan kidogo yakanifanya nishikwe na bumbuwazi huku nikimtazama usoni mwake, kwani haya anayo nieleza sijawahi kuyafikiria kabisa kwenye akili yangu.



“Nani amepanga kunibambikia kesi?”

“Utajua, ila ukweli ni kwamba huyu si mama yako. Kitu kingine ninacho kihitaji Ethan sasa hivi usifanye maamuzi makubwa pasipo kunishirikisha. Muda mwengine ninakuja kukusaidia kwa sababu wewe ni rafiki yangu, ila nikiama kukaa mbali nawe basi nitakaa na utashindwa kwneye kila jambo. Umenielewa?”

Ethan alizungumza kwa msisitizo huku akinitazama usoni mwangu.

“Nimekuelewa kabisa sinto rudia makosa”

“Yaa napenda kusikia hivyo. Sasa hivi nenda katafute hoteli, lala kesho urudi kambini”

“Sawa”

Ethana akapotea na kuniacha peke yangu katika chumba hichi. Nikamtazama mwana mama huyu kwa macho makali sana, nikatoka ndani humu na nikakutana na Camila mlangoni.

“Vipi mume wangu”

“Twende zetu hotelini”

“Hotelini tena?”

“Ndio, nahitaji kwenda kupumzika”

“Ila mbona kama unaonekana kama umekasirika”

“Twende nyumbani”

Nilizungumza kwa msisitozo mkali sana na kumfanya Camila kukubaliana na kile nilicho mueleza. Tukatoka katika eneo hili na walinzi wawili wakatangulia mbele yetu huku walinzi wengine wawili wakiwa nyuma yetu. Wakatufunguli mlango wa gari na tukaingia ndani kisha taratibu tukaanza kuondoka katika eneo hili.

“Ethana mbona sijakuelewa kabisa, kwa nini umetaka tumuache mama pake yake kule hospitalini?”

“Sio mama yangu”

“Samahani, sijakuelewa?”

“Si mama yangu, hujanielewa nini?”

Nilizungumza kwa hasira kidogo na kumfanya Camila kukaa kimya. Camila akawaelekeza walinzi watupeleke katika hoteli nzuri na yenye ulinzi. Tukafika katika hoteli yenye hadthi ya nyota tano, Camila akatumia kadi yake maalumu ya malipo kulipia moja ya chumba cha kisasa kisha tukaelekea ndani.

“Ethan muda ule nilishindwa kuliongelea hili swala kwa urefu. Hembu niambie yule si mama yako kivipi, ikiwa ulisha sema ni mama yako?”

“Kuna mchezo ambao unachezwa hapa na wajinga”

“Mchezo gani?”

“Hadi hivi sasa mimi siukumbuki. Nimeweze kumtazama yule mama na kutafuta alama ambazo nilikuwa ninamuona nazo mama yangu, ila sijafanikiwa kuweza kuziona, hivyo wana nidanganya”

Ilibidi nimuongopee Camila.

“Mmmm ni kina nani hao lakini?”

“Si wale jamaa?”

“Jamaa wapi?”

“Mmoja wao ni yule mzee amabaye alinionyesha picha za huyu mwana mama akiniaminisha kwamba ni mama yangu ila ukweli ni kwamba si mama yangu”

“Mmmmm”

“Ndio Camila, kuna watu wana mpango wa kunifilisi na kunibamikia makesi ya ajabu. Endapo nitawajua haki ya Munu nitafaja jambo moja baya snaa kwao”

“Mume wangu usiipe hasira nafasi ya kutawala moyo wako. Tafadhali na nakuomba uwe mvumilivu. Naamini huko mbeleni tutajua ni nani mbaya kwako na nani ni mzuri kwako. Ila tafadhali nakuomba uwe makini na kila mtu wa karibu yako”

“Ikiwemo wewe”

Jibu langu likamduwaza Camila, nikavua viatu na kujitupa kitandani. Mwili wangu kwa namna moja ama nyingine umechoka sana, toka asubuhi sikuweza kupata hata muda mzuri wa kupumzika. Camila taratibu akapanda kitandani huku akiwa mnyonge sana.

“Ethan”

“Mmmmm”

“Natambua ya kwamba una huzuni kubwa sana moyoni mwako. Natambua kwamba kitendo nilicho kufanyia hadi sasa hivi bado hakijafutika akilini mwako. Ila tambua kwamba kila jambo nililo kuwa nimelifanya kwako kwa kipindi cha nyuma hazikuwa akili zangu. Nakuomba unisamehe Ethan”

“Nimekusamehe. Tule tulale”

Camilaakaandaa chakula huku akionyesha dhairi kwamba hana furaha kabisa. Tukapata chakula, tukaingia bafuni kwa pamoja, tukaoga kisha tukarudi chumbani na kulala pasipo hata mmoja kudhubutu kunyanyua hisia za mwezake.

Asubguhi na mapema tukaanza safari ya urudi kambini. Msafara wa gari hizi tatu huku gari letu likiwa katikati, ukazidi kusonga mbele. Meseji ikaingia kwenye simu yangu. Nikaifungua na kukuta ikiwa imetoka kwa mwanasheria.

‘NIPO HOSPITALINI MADAKTARI WANADAI HAUPO MKUU, UPO WAPI?’

Nikaitazama meseji hii kwa muda, kisha nikampigia mwana sheria.

“Ndio mkuu za asubuhi?”

“Salama, sasa ni hivi”

“Ndio”

“Hakikisha unasimamia matibabu ya mwana mama huyo hadi anapona. Kisha arudishwe nchini Tanzania akaendelee na maisha yake”

“Ahaa….samahani mkuu, kwa nini umechukua maamuzi hayo?”

“Ni maamuzi yangu binafsi nahitaji akipona. Umpatie dola elfu hamsini, akaanzie maisha Tanzania. Mambo mengine nitakueleza muda ukifika wa kuyazungumza”

“Sawa mkuu nimekuelewa”

“Nashukuru”

Nikakata simu na kuirudisha mfukoni.

“Ethan”

“Mmmm”

“Haya maisha yetu ya kukaa kimya ya kuto kuzungumza, kununiana hakika mimi siyapendi mume wangu”

“Kwani Camila nimekununia?”

“Ndio, jana usiku, tumelala kila mtu amegeukia kwake. Leo asubuhi, tumeamka hata busu la hasubuhi hatukupeana, kila mmoja ameamua kufanya anacho taka kwa nini lakini”

Camila alizungumza kwa sauti iliyo jaa malalamiko, nikawatazama walinzi wawili walio kaa siti ya mbele huku mmoja akiwa ni dereva.

“Sijakukasirikia mke wangu, ila ninakasirika huu mchezo unao endelea”

“Sawa, ila tambua kwamba mimi ni mke wako”

“Natambua hilo na nitazidi kulitambua, ila na wewe unatakiwa kunibembeleza ukiniona nikiwa katka hali kama hii”

“Nitakubembeleza vipi ikiwa mwenyewe unanijibu vibaya”

“Sa…..”

Hata kabla sijaimalizia kauli yangu, dereva akayumbisha gari letu, huku akilikwepa gari la mbele lililo tutatungulia ambali, tunalishuhudia jinsi lilivyo paishwa angani kwa kulipuliwa na bomu moja kubwa na likatua chini na kusambaratika. Dereva wa gari letu akajitahidi kwa kadri ya uwezo wako kuliweka gari sawa, huku dereva wa gari la nyuma, akitutipa kwa kasi sana na kutangulia mbele yetu. Gari hizi mbili zilizo salia zikasimama, huku eneo hili tulilopo ni eneo la barabara za juu, katikati na chini. Ubaya wa barabara yuliyopo ni katikati, eneo ambalo huwezi kujirusha kwenda sehemu yoyote.

Watu walio valia nguo nyeusi, huku wakiwa na pikipiki kubwa, wakasimama mita kadha kutoka gari hizi zilipo na wakaanza kuzishambulia.

Walinzi kama jukumu lao la kutulinda, wakaanza kushuka kwenye magari haya na kujibu mashambulizi. Mimi na Camila miili yetu ina tetemeka kupita maelezo.

“Ohoo Mungu wangu”

Nilizungumza huku nikiendelea kushuhudia jinsi walinzi wanavyo zidi kupungua. Kwa haraka nikafungua mkanda wa siti niliyo kalia na kuahamia siti ya mbele ambayo mlinzi wake ameshuka kupambana na wavamizi hawa.

“Unafanyaje Ethan?”

Camila alizungumza huku akimwagikwa na machozi usoni mwake.

“Kaa hapo hapo”

Nilizungumza, huku nikikaa kwenye siti ya dereva ambaye tayari amepigwa risasi ya kichwa na kufa. Wavamizi wakazidi kutusogelea huku wakizidi kuwapukutisha walinzi wetu. Mlinzi aliye salia naye akapigwa risasi na kutufanya tubaki sisi kama sisi.

‘Lazima nifanye jambo hapa’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikifunga mlango ambao alishuka mlinzi. Nikaokota bastola moja ya dereva, kisha nikaufunga mlango kwa nguvu. Risasi zinazo pigwa kwenye kuelekea lilipo gari letu haziingii ndani ya gari kutokana gari hili limetengenezwa kwa mfumo wa kuto kuingiza risasi.

“Ethan unafanya nini mume wangu”

“Lala kwenye siti”

Nilizungumza huku nikilirudisha gari hili nyuma, mnikaligeuza kwa kasi sana hadi likakaribia kuaguka. Nikaingiza gia namba moja gari likanza kusonga mbele taratibu, nikazidi kuongeza gia za garihili na kulifanya lizidi kuongezeka mwendo. Kupitia kioo cha pembeni, nikashuhudia kuona wavamizi hawa wenye pikipiki zipatazo saba wakituandama huku kwenye kila pikipiki wakiwa wamepanda wawili wawili. Camila akajaribu kuchungulia ila kwa jinsi kioo cha nyuma kinavyo shabuliwa kwa risasi na kusababisha alama nyingi nyingi, nikajikuta nikimfokea Camila na kumuomba alale chini. Sikuwa na budi ya kukwepa magari ninayo kutana nayo, kwani barabara hii inaruhusu magari ya kwenda upande mmoja tu ambao tulikuwa tunauelekea.

“Ni kina nani Ethan?”

“Sifahamu Camila”

Risasi zikazidi kumiminika na mbaya zaidi watu hawa ni wataalamu wa kuendesha pikipiki, kisha cha kunifanya hata niendeshe gari vipi, wana zidi kunisogelea.

‘Ethan naomba msaada wako’

Nilizungumza kimoyo moyo, ila sikuweza kupata msaada wowote wa Ethan. Nikafika katika barabara ya kugeza ambayo inapita eneo la chini, nikakanyaga breki kidogo, huku nikikunja kona hii kali na kulifanya gari liserereke, na kujibamiza kwenye vymba vikubwa vilivyo jengewa pembezoni mwa barabara hii kisha likaa sawa na tukaondoka katika eneo hili kwa mwendo wa kasi.

“Ethan”

“Mmmm”

“Naomba bastola”

“Bastola ya nini?”

“Kuna hawa wanatusogelea?”

Camila alizungumza huku akijipangusa machozi usoni mwake. Nikatazama kioo cha pembeni yangu nan ikawaona wavamizi wawili wakiwa wanatukaribia kabisa. Nikafunga breki za gafla na kuwafanya mmoja wao kugonga pipiki hii kwa nyuma na kusababisha ajali moja mbaya sana.

“Njoo uendeshe”

Nilizungumza huku nikuhamia siti ya nyuma kwa haraka, tukapishana na Camila kama upepo kwani hapa tunapigania maisha yetu kama wapenzi. Akaka kwenye siti ya dereva kisha akaliondoa gari hili kwa kasi sana. Nikaikoki bastola hii vizuri huku nikitazama pikipiki zinazo kuja. Kioo hichi cha nyuma hakika kimejaa alama nyingi za risasi hadi zinasababisha kuto kuweza kuona vizuri nyuma na kimebakisha asilimia ndogo sana kitoboke na kuruhusu risasi kuweza kuingia ndani ya gari hili.

“Ongeza mwendo Camila”

“Najitahidi”

Nikafungua kioo kidogo kisha nikautoa mkono wnagu wa kushoto ulio shika bastola na nikaanza kufyatua risasi kadhaa kuelekea nyuma.

“Ethana una fanya nini!?”

“Nawazui wasitukaribie”

“Ohoo Mungu wangu”

Camila alizungumza huku akijitahidi kufunga breki za gari hili hadi nikarumbishwa na kujipigiza katika siti pembeni yangu. Nikatazama mbele na kushuhudia lori moja kubwa sana likiwa limeziba njia na mbaya sana zaidi tupo kwenye barabara aina ya karabati na eneo hili linawashwa taa masaa ishirini na la sivyo kuna kuwa na giza moja zito sana.

“Ni mtego mpenzi wangu”

Nilizungumza huki nikikaa sawa, nikafunga kioo nilicho kuwa nimekifungua kidogo. Juu ya lori hili tukaona watu wawili nao wakiwa wamevalia nguo nyeusi huku mikononi mwao wakiwa wameshika mabomu aina ya bazooka ambayo laiti wakiyafyatulia kwenye gari letu basi, gari litanyanyuliwa kama vile lilivyo nyanyuliwa gari la walinzi wetu lililo kuwa limetangulia mbele.

“Camila”

“Mmmm”

“Usifanye kitu chochote hawa watu wanahitaji sisi tukiwa wazima”

“Ethan tuna kufa mume wangu”

“Hatuwezi kufa, niamini mimi na tutoke kwenye gari”

Nilizungumza huku nikishuhudia wavamizi wenye pikipiki wakisimamisha pikipiki zao nyuma yetu. Ubaya watu hawa wamejifunika sura zao jambo la kushindwa kumtambua nani ni nani. Wakatuamrisha kushuka kwenye gari huku mikono yetu ikiwa ipo juu. Nikamkonyeza Camila nikimuashiria tufanye kama tulivyo agizwa, kwa haraka Camila akaninyonya lipsi zangu huku machozi yakimwagika usoni mwake, taratibu na mimi machozi yakaanza kunimwagika. Nikazitoa lipsi zangu kwa Camila kisha nikafungua mlango wa gari hili na nikawa wa kwanza kushuka huku watu hawa wakianza kunisogelea kwa ukaribu sana, akafwatia Camila naye akashuka huku akitetemeka sana. Jamaa hawa wakatunyooshea mitutu yao ya bunduki, wakazikoki vizuri tayaru kwa kutuua jambo lilizo tufanya tuzidi kujawa na hofu kubwa sana



Mmoja wa watu hawa akanisogelea na kunipokonya bastola niliyo ishika huku mikono yangu ikiwa juu. Akanipiga kwa kutumia kitako cha bunduki kifuani mwangu na kujikuta nikianguka chini mzima mzima huku nikihisi maumivu makali sana. Wakamvisha Camila kigunia cheusi kichwani mwake huku wakimfunga mikono yake na pingua, japo Camila alijitahidi kurusha rusha miguu na mikono yake, ila hakuweza kuzuia watekaji hawa kutimiza azima yao. Wakaninyanyua na mimi, jamaa mmoja akanipiga ngumi ya kifuani mwangu na kujikuta nikigugumia kwa maumivu makali sana. Wakanifunga mikono yangu kwa nyuma kwa kutumia pingu, kisha nami wakanivisha kigunia cheusi ambacho kikanizuia kuweza kuona ni kitu gani ambacho kinaendelea. Nikasukumiwa ndani ya gari ambalo sifahamu ni gari gani.

“Camila, Camila”

Niliita ila nikastukia nikipigwa teke la kifuani mwangu.

“Kaaa kimya pumbavu wewe”

Niliisikia sauti ya kiume ikifoka, sikuhitaji kuendelea kupata matatizo zaidi ya kuendelea kukaa kimya kwa maana watu hawa sihitaji waendele kunidhuru zaidi.

‘Ethna upo wapi rafiki yangu’

Nililamama huku nikiwa nimelala chini kwa kujikunja ndani ya gari hili ambalo inaonyesha ni lori kubwa sana. Baada ya kama ya saa moja na nusu, nikasikia breki za lori hili, likasimama, watu hawa walio tuteka wakanikamata mikono yangu, wakaninyanyua na kunishusha ndani ya lori hili. Nikaanza kutembezwa mkuku mkuku, nikakalishwa kwenye moja ya kiti kisha kigunia nilicho vishwa kichwani mwangu nikavuliwa. Mwanga mkali wa taa yenye mwanga mweupe ikanipiga machoni mwangu, jambo lililo sababisha niyafumbe macho yangu kwani ni maaumivu makali sana ninayo yapata yatokanayo na mwanga huo. Baada ya kumulikwa na taa hizi zenye mwanga mkali kama dakika tano hivi, wakazizima na kuyafanya macho yangu kujaa mawenge mawenge mengi kidogo.

Nikamuona Camila akiwa amekalishwa kwenye kiti cha mbele yangu huku akimwagikwa na machozi mengi sana usoni mwake. Mdomoni mwake wamamfunga kitambaa cheusi ambacho sio rahi kwa yeye kuweza kutoa sauti. Pembeni yake wamesimama watu wawili walio shika mitutu ya bunduki.

“Halooo Ethan”

Nilisikia sauti mbaya na nzito ikizungumza huku ikitokea kwenye kipaza sauti kidogo kilicho fungwa pembeni yetu.

“Munataka nini nyinyi wana haramu?”

Nilizungumza kwa hasira huku nikijitahidi kujitoa mikono yangu kwenye pingu hii.

“Hahaaaa……ni jambo dogo sana tunataka kutoka kwako”

“Zungumzeni basi nipo tayari kuwapatia, ila mke wangu awe salama”

“Hahaaaa…..mke wako hausiani na kile ambacho tunakihitaji kutoka kwako”

“Tunahitaji boksi jeusi na Camila tunahitaji baba yako asigombanie uraisi wa hii nchi, ahakikishe anajitoa kwenye kinyang’anyiro hichi mara moja la sivyo tutaikata shingo yako”

Sauti hii iliendelea kutoa kauli ambazo hakika zinatisha.

“Niueni ila sifahamu ni wapi lilipo boksi jeusi”

“Ohoo tukuue”

“Ndio”

Camila akaanza kutingisha kichwa huku akigugumia kwa kulia, maamuzi nilio amua kuyachukua ni magumu sana. Maamuzi ambayo hakika yatamuacha na upweke katika kipindi chote cha maisha yake.

“Mpigeni risasi afe”

Sauti hiyo ilizungumza na watu wawili wakasimama mbele yangu huku wakiwa wameshika mitutu yao ya bunduki.

‘Nimekuja’

Niliisikia sauti ya Ethan ndani yangu, mwili wangu ukapata msisimto mmoja wa ajabu, pingu nilizo fungwa mikono mwangu zote zikakatika, nikasimama kwa haraka sana, nikawawahi watu hawa wawili, kwenye shingo zao, nikawanyanyua juu kwa mikoano yangu, kisha nikawarusha walipo simama watu walio mzingira Camila na kusababisha watu wengine kuanza kunishambulia kwa risasi. Kasi iliomo mwilini mwangu na uwezo alio nipatia Ethan, ukanifanya niweze kukwepa risasi zote ambazo wananishambulia.

Nikazivunja pingu za Camila za mikononi na nikaifungua miguu yake kisha yeye akamalizia kufujifungua kitambaa cha mdomoni mwake. Camila hakuhitaji kuwa mzembe, akaokota moja ya bunduki na kuanza kuwashambulia watu wengine huku nami nikiwa na kazi ya kutumia nguvu nilizo pewa na Ethan kuwanja vunja viuongo vyao watu hawa. Ndani ya dakika tano watu wote waliomo ndani ya holi hili, tukawabadilisha majina na kuwa ni marehemu. Camila akanikumbatia kwa haraka huku akiwa analia.

“Imekwisha baby”

Nilizungumza huku nikiendelea kumkumbatia Camila kwa nguvu sana.

‘Muhusika ana kimbia toka nje’

Niliisikia sauti ya Ethan, nikamuachia Camila na kwa haraka nikaanza kukimbia kueleekea nje, nikakuta gari moja nyeusi aina ya Lexus ikioandoka kwa kasi eneo hili, nikaangza huku na huku na nikaona moja ya pikipiki. Nikaifwata na kwa bahati nzuri nikakuta ikiwa na funguo, nikaiwasha kabla ya sijaondoka, nikamuona Camila akitoka katika holi huku akiwa na bastola mbili mikononi mwake.

“Njoo upande”

Nilimuambia huku nikitazama gari hii jisni inavyo timua vumbi. Camila kwa haraka akaokota heliment mbili za pikipiki, akanirushia moja kisha naye akavaa jengine, na kupanda kwenye hii pikipiki. Nikatia gia na kuanza kufukuzia gari hili. Uzuri wa pikipiki hii ina ina spidi mita mia mbili na ijini yake ni kubwa kiasi cha kuifanya iweze kushindana mwendo kasi na gari hili linalo zidi kwenda kwa kasi katika barabara hii ya vumbi.

“Ongeza mwendo”

Camila alizungumza huku akiwa ameizungusha mikono yake kiunoni mwangu.

“Poa poa”

Nilizungumza huku nikiongeza mwendo kasi wa pikipiki hii kutoka mia moja na stini hadi kuanza kukaribia spidi mita mia mbil, jambo lililo sababisha taa ndogo nyekundu kuanzza kuwaka pembeni ya dashbod ya spidimita.

Tukaanza kulikaribia gari hili, Camila akanishika mkono mmoja kiuno changu, huku mkono wake mwengine akiuweka begani mwangu huku akiielekezea bastola aliyo ishika kwenye gari hilo. Akaanza kufyatua risasi kadhaa kueleke kwenye gari hilo, baadhi ya risasi zikazipiga gari hili kwa nyuma na kusababisha lianze kuyumba na likapoteza dira na kuvamia miti iliyopo pembezoni mwa eneo hili ambalo ni nje kabisa ya mjini. Nikaanza kupunguka mwendo mara baara ya kulishuhudia gari hili likipinduka matairi juu kichwa chini. Nikasisimamisha pikipiki hii mita chache kutoka eneo la ajali, tukashuka huku tukivua heliment za pikipiki hii.

“Nisubirie hapa”

Nilimuambia Camila huku akinikabidhi bastola moja.

“Etha…..”

Nikamtazama kwa macho makali ambayo yaliweza kumpa ishara ya kunyamaza kimya. Nikaanza kutembea kwa umakini sana kuelekea kwenye gari hili, nikamuona dereva akijivuta pembeni akitokea kwenye gari hili huku akiwa analalamika maumivu ya kuvujika mguu. Nikachungulia siti ya nyuma napo nikaona kuna mtu, nikamfungua mlango wa gari hili na kuanza kuivuta miguu ya mtu huyu ambaye sura yake bado sijaiona.

Nikastuka sana mara baada ya kuiona sura ya mwanasheria wa kampuni zangu. Mtu ambaye nimemuamini kwa maisha yangu. Mtu ambaye anafahamu siri zangu nyingi sana na hata baadhi ya makampuni yangu anayaongoza yeye.

“Nilikuambia utulie utaona, umejionea sasa?”

Ethan alizungumza huku akiwa amekaa pembeni yangu. Mwili mzima nikaihisi ukinyon’onyea sana. Camila uvumilivu ukamshinda na nikaanza kumuona akija katika eneo hili.

“Camila atakuona”

“Yaa inabidi anione, bila mimi musinge kuwepo hapa. Naamini leo ndio mara yake ya pili ataniona”

Ethan alizungumza huku tukimtazama Camila aliye karibia kufika hapa. Camila alipo muona Ethana, kwa haraka akamnyooshea bastola.

“Ondoka pembeni ya mume wangu”

Camila alizungumza kwa ukali sana na kumfanya Ethan kuangua kicheko kikubwa kilicho jaa kejeli ndani yake.

“Nimesema ondoka nitakuua”

“Camila tulia”

“Siwezi kutulia huyo ndio muuaji. Aliwaua walinzi wangu siku ile”

“Ndio niliwaua, unataka kuniua na mimi si ndio”

“Nimesema usinijaribu, nitakuua”

Ethan kwa haraka akasimama mbele ya Camila jambo lililo nifanya nihitaji kupiga hatua moja mbele ila nikagundua adui yangu hadi sasa hivi sijajua amepoteza maisha au amezimia.

“Camila acha, huyu ni fariki yangu na yeye ndio aliye nipatia msaada kwenye maisha yangu”

Nilizungumza kwa msisitizo huku nikimtazama Camila usoni mwake. Uso nzima wa Camila umebadilika na kuwa mwekundu kwa hasira.

“Tafadhali mke wangu, sikikilize basi achana na Ethan njoo ushuhudie hili hapa”

“Msikilize mume wako, kwa maana mimi huwezi kuniua kwa maana si binadamu.”

“Si binadamu?”

“Wote acheni ujinga”

Ilinibidi nizungumze kwa kufoka na kuwafanya Camila na Ethan kunitazama.

“Tuna kazi ya kufanya, nahitaji kujua huyu mshenzi kama yupo hai au amekufa. Nyinyi mumekalia upuuzi sitaki ujinga”

Niliendelea kuzungumza kwa kufaka na kumfanya Camila kuishusha bastola yak echini taratibu. Nikakitazama kifua cha mwana sheria na nikakiona kikihema taratibu.

“Mpuuzi yupo hai huyu”

Nilizungumza huku nikimalizia kumvuta kutoka ndani ya gari. Nikamtazama dereva anaye endelea kulia kwa maumivu makali anayo yahisi. Nikamsogelea na kuchuchumaa pembeni yake.

“Unahisi maumivu si ndio?”

“Ehee….nisaidie….nisaidie tafadhali”

Nikasokomeza bastola yangu mdomoni mwake, akanitolea macho ya woga sana huku akinitazama usoni mwake. Nikafyatua risasi mbili mfululizo na kumfanya kichwa chake kichanguke kwa nyuma na damu zikaanza kutapakaa kwenye mchanga. Taratibu nikaichomo bastola yangu na kurudi eneo alipo mwana sheria ambaye amezungukwa na Ethan pamoja na Camila ambaye anashanga uwepo wa mwana sheria huyu katika eneo hili.

“Ethan huyu si mwana sheria wako?”

“Ndio”

“Mbona yupo hapa?”

“Yeye ndio anahusika kwa kila kitu ulicho kiona leo”

“Ohoo Mungu wangu!!”

“Ethan unaweza kumuamsha?”

“Mmmmm nina weza”

“Muamshe”

Ethan akamshika mwana sheria eneo la shingoni mwake. Taratibu mwanasheria akafumbua macho yake. Ethana akamshika shat lake eneo la kufuani mwake na kumkalisha kitako huku akimuegemeza kwenye gari hili lililo pata ajali. Mwanasheria woga mwingi sana ukamtazama, hakutegemea kutuona hapa sisi watatu, kwa hasira niliyo nayo hadi nikajikuta nikikosa cha kuzungumza na mkono nilio shika bastola ukaanza kutetemeka.

“Kwa nini umefanya hivi?”

Nilijikaza kuzungumza ila mwana sheria akakosa cha kunijibu zaidi ya machozi kuendelea kumwagika.

“Haya ndio aliyo kuagiza baba yangu uyafanye juu yangu si ndio?”

“N…..i…nii same….he…..Ethan”

Mwanasheria alizungumza huku akimwagikwa na machozi usoni mwake.

“Ethna nimefanya hivi kwa ajili ya familia yangu, kwa ajili ya mke wangu na mwanangu”

“Mke wako na mwanao ndio walio kuagiza kuniteka mimi na Camila na kunishinikiza vitu vya kijinga si ndio?”

“A….a…..!!”

Mwanasheria kigugumizi kikaendelea kumbana kifuani mwake.

“Nakuuliza mke wako ndio aliye kuagiza kufanya ujinga huu si ndio?”

“Nd….ndi….ooo”

“Mke wako ndio aliye taka utuue sisi na mume wangu, jamani mbona hana huruma. Tumemfanyia nini jamani ehee?”

Camila alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake.

“Mke wangu anagombania kiti cha uraisi hawa pia ni watu wake aio nikabidhi kufanya nao kazi. Alinishawishi sana nikushawishi umuunge mkono, ila nikakataa ndio maana akatumia nguvu hii.”

“Ina maana bi Magnalena Schoss ni mke wako?”

Camila aliuliza huku akimtazama mwana sheria usoni mwake.

“Ndio ni mke wangu na tuna miaka thelethini sasa katika ndoa”

“Boksi jeusi alilihitaji la nini kwangu?”

“Eheeeee!!!”

Mwanasheri alijifanya kama hajasikia, nikampiga na kitako cha bastola kwenye ugoko wa mguu wake wa kushoto na kumfanya alie kwa uchungu sana huku akinitazama usoni mwangu.

“Alihitaji boski jeusi kwa ajili gani?”

“Ni kwa ajili ya kujihimarisha kiusalama zaidi”

“Ahaa…..sawa sawa”

Nilizungumza huku nikiikoki bastola yangu na kumuelekezea kichwani, kama alitoa amri ya mimi kupigwa risasi basi na yeye hana nafasi ya kuishi hapa duniani.

“Ethan ngoja kwanza usimuue”

Ethan alizungumza huku akinitazama.

“Kwa nini?”

“Kwa kumtumia huyu basi tutahakikisha huyo mwana mama anaenguliwa katika kasi za kugombania uraisi na itazidi kumpa nguvu baba mkwe wako kushinda uchaguzi wa uraisi”

Ethna alizungumza kwa upole, kabla sijafanya chochote simu ya mwanasheria huyu iliyopo kwenye koti lake la suti ikaanza kuita, nikampasa kwa haraka na nikaitoa. Nikakuta namba hiyo ni ya mke wake, nikamuonyesha kisha nikaipokea na kuiweka sikioni mwangu.

“Mume fiki wapi mume wangu. Nipe habari njema”

“SIO HABARI NJEMA, NI HABARI MBAYA MUME WAKO AMEFARIKI DUNIANI”

Nilizungumza kwa sauti nzito na iliyo jaa mikwaruzo mingi sana na kumfanya mwana mama huyo kukaa kimya kwa sekunde kadhaa akisikilizia sauti yangu.



“JIANDAE NINAKUJA KWA AJILI YAKO”

Baada ya kumaliza kuzungumza maneno hayo nikakata simu huku nikimtazama mwanasheria wangu aliye amua kunisaliti kwa ajili ya mke wake.

“Ngoja nikachukue gari”

Ethan alizungumza huku akiondoka katika eneo hili. Mwanasheria hakuzungumza kitu chochote zaidi ya kuendelea kumwagikwa na machozi usoni mwake.

“Endapo nitagundua umefanya udanganyifu kwenye kitu chochote ndani ya kampuni yangu. Ninakuapia kwa jina la marehemu yangu. Lazima nitakua, umenielewa wewe mpuuzi”

Mwanasheria akazidi kulia kwa uchungu sana huku akionekana kujutia kwa maamuzi ya kijinga aliyo yafanya.

“Mke wako kwa nini amekuwa na roho mbaya kiasi hichi ehee?”

Camila alimuuliza mwanasheria, ila mwanasheria akaishia kumtazama Camila tu.

“Ila Mungu ni mwema, unakumbuka jana nilikuambia tuondoke pale hospitalini?”

“Ndio”

“Na nilikueleza kwamba yule sio mama yangu”

“Ndio”

“Niliustukia mpango wa huyu mzee. Yaani sijui ulikuwa uanichukuliaje. Kumbuka nimebakisha siku kumi tu kuingia umri wa miaka kumi na nane sasa wewe endelea kuleta ujinga wako mzee. Mimi sio mtoto na hata nikiwa katika umri huu huwezi kunidanganya. Mjinga wewe”

Tukamuona Ethan akisimamisha gari katika eneo lenye barabara. Akashuka na kutufwata sehemu hii tulipo. Akamnyanyua mwanasheria wangu na kumfunga pingu za mikononi mwake. Akampeleka moja kwa moja kwenye gari na kumuingiza siti ya nyuma huku nasi tukiwa nyuma yao.

“Mjini kwa sasa kila sehemu ina kaguliwa na askari kuwatafuta nyinyi mulipo, kwani habari ya kutekwa kwenu imesambaa kila mahali. Sawa”

“Sawa je wewe uungani nasi?”

Camila alizungumza huku akimtazama Ethan usoni mwake.

“Hapana mimi nitaondoka na hii pikipiki”

“Sawa”

“Ila angalizo, hakikisheni kwamba munampeleka katika sehemu ambayo itakuwa ni salama kwa nyinyi kumshikilia kwa kipindi chote katika kuhakikisha kwamba muna muangusha mke wake katika kumtoa katika kinyang’anyiro cha kuiongoza nchi hiyo.”

“Sawa nimekuelewa”

“Ila nitaendelea kuwalinda kwa ukaribu na sasa hivi Ethan hakikisheni kwamba kila hatua ya jambo linalo watatiza munaipiga na nitakuwa pamoja nanyi. Mumenielewa”

“Sawa”

“Shemeji safari jema”

“Nashukuru”

Tukaingia kwenye gari siti za mbele. Camila akaishika bastola yake na kumuelekezea mwanasheria aliye kalishwa siti ya nyuma. Nikawasha gari hili na kuanza kuondoka katika eneo hili kwa mwendo wa kasi. Kutokana gari hili lina GPRS haikuwa tabu kwa sisi kuusaka mji wa Berilin amboa ndipo tunapo ishi.

“Baby”

“Mmmm”

“Yule umesema anaitwa Ethan?”

“Ndio”

“Ni mtu kweli?”

Nikamtazama Camila usoni mwake, kisha nikatingisha kichwa nikimaanisha kwamba sio mtu. Camila akanielewa jibu langu huku akinitazama machoni mwangu.

“Ethan”

Mwanasheria aliniita kwa sauti ya upole na iliyo jaa unyenyekevu, nikamtazama kwa kupitia kioo kidogo kilichopo juu upande wangu wa kulia.

“Ehee”

“Vita ulio ingia ni kubwa sana mwanangu. Ninakuonea huruma kubwa sana”

“Pumbavu wewe nyamaza. Unahisi kwamba ninaogopa. Kama ulishindwa kuniua leo basi tambua kwamba hamuto niweze kuniua hata siku zijazo. Hata mukija watu laki, Mungu yu pamoja nami na hamutoweza kufanya lolote kwangu”

Nilizungumza kwa kujiamini sana huku nikiendelea kuendesha gari hili kwa kasi.

“Natambua hilo ila vita hii amekuachia baba yako mzee Klopp”

“Eti ehee?”

“Ndio, mali alizo zulimu, watu alio waua kipindi cha uhai wake. Damu zao zipo mikononi mwako, kwani wewe ndio mrithi wa mali zake. Leo hii umenionyesha na wewe una ukatili kama wa baba yako kwa maana umemuua dereva wangu ambaye hakuwa na hatia yoyote kwenye hili swala”

Nikayafumba macho yangu kwa sekunde kadha kisha nikafunga breki za gafla hadi Camila akashangaa. Nikashuka kwenye gari na kufungua mlango wa siti za nyuma, nimatoa mwana sheria kwa nguvu na kumbwaga chini. Nikaanza kumpiga mateke ya tumboni mwake huku nikimtukana matusi ya kila aina.

“Baby baby acha tafadhali”

Camila alizungumza huku akanisogeza pembeni kwani mateke niliyokuwa ninampiga mwana sheri kwa hakika yanaweza kumsababishia kifo.

“Mume wangu tuliza jazba kidogo. Kumbuka huyu mzee tunamuhitaji katika haya mapambano. Unavyo endelea kumpiga hivyo utazidi kumsababishia matatizo na mwishowe atakufa sawa mume wangu”

Camila alizungumza huku akiwa amenishika mashavu yangu. Akanibiga busu moja matata mdomoni mwangu, busu hili taratibu likazifanya hisia zangu za hasira kuanza kushuka taratibu na nikarudi katika hali yangu ya kawaida.

“Tambua nina kutegemea sana mume wangu. Tambua hii vita ni ya kwetu wote. Maisha ya baba yangu yapo hatiana na hata familia yangu kwa sasa ipo mashakani. Tafadhali ninakuomba mume wangu uwe mpole sawa baba”

“Nimekuelewa mke wangu”

Nilizungumza kwa upole kisha nikamnyanyua mwanasheria na kumuingiza ndani ya gari. Tukaendelea na safari hii huku akilini mwangu nikifikiria ni sehemu gani ambayo ninaweza kumpeleka huyu mwana sheria. Taratibu nikapunguz amwendo wa gari na kulisimamisha pembezoni mwa barabara.

“Huyu mtu mjini hatuwezi kumpeleka mke wangu ni hatari”

“Kweli ni hatari mume wangu, nami nilikuwa ninaliwaza jambo hilo ila nikashindwa tu kukuanza”

“Hufahamu sehemu yoyote ambayo tunaweza kupata nyumba ya kumhifahdhi huyu shetani?”

“Mmmmm sifahamu”

Tukiwa katik ahali ya kujiuliza maswali ya hapa na pale, tukaanza kuona helicopter mbili za jeshi la nchi hii ya Ujerumani zikija mbele yetu. Nikakata kuwasha gari ila Camila akanizuia.

“Wamekuja kwa ajili yetu hawa”

“Una uhakika?”

“Ndio mume wangu, naamini kwa kutumia satelaiti wameweza kufahamu sehemu tulipo”

“Umejuaje?”

“Kumbuka hata kwa kupitia sura zetu tunaweza kutafutwa na kujulikana ni wapi tulipo na mbaya zaidi pale ulipo shuka kwenye gari na kuanza kumuadhibu huyu mzee nayo pia imechangia”

Camila alizungumza huku tukishuhudia helicopter hizo zikianza kusimama taratibu mita kadhaa kutoka sehemu ilipo gari letu. Wakashuka wanajeshi zaidi ya kumi na mbili, taratibu tukashuka kwenye gari hili. Wanajeshi hawa wakafika katika eneo hili.

“Ninaitwa Camptein Gudluck, kutoka jeshi la anga. Tupo hapa kwa ajili ya kuwaokoa.”

Mwanajeshi mmoja alizungumza huku akitupa mikono.

“Mumefahmu vipi kwamba tupo hapa?”

Nilimuuliza mwanajeshi huyu huku nikimkazia macho usoni mwake.

“Kupitia satelaiti”

Mwanajeshi huyu alizungumza huku akinionyesha alama ndogo inayo onekana kwenye simu yake aina ya iphone 6. Mapigo ya moyo yakanistuka mara baada ya kuona chata ndogo kwenye mkono wa mmoja wa huyu mwanajeshi. Chata hii ikanikumbusha vijana wa mwanasheria ambao aliwaagiza kwenda kunitafutia mama yangu nchini Tanzania.

‘Ohoo Mungu wangu, tumeingia tena mikono ni mwao’

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikimkanyaga Camila kwenye mguu wake. Gafla helicopter moja ikalipuka na kutuchanganya watu wote katika eneo hili.

“Rudi kwenye gari”

Nilimuambia Camila kwa sauti ya ukali. Camila hakuhitaji kupoteza muda, kwa haraka akarudi kwenye gari huku nami nikirudi kwenye gari. Nikaliwasha gari hili na kuanza kulirudisha nyuma na kuwafanya wanajeshi hawa kuendelea kutushambulia kwa risasi.

“Mungu wangu ni kina nani wale!!?”

Camila alizungumza huku akiwa amejawa na mstuko mkubwa sana.

“Ni watu wa huyu mzee”

“Ohoo samahani mume wangu kwa kukuamisha kwamba ni watu wa serikali. Tukashuhudia helicopter nyingine nayo ikilipuka mlipuko mmoja mkali sana. Wanajeshi wanao tushambulia tukawashuhudia jinsi wanavyo anguka mmoja baada ya mwengine.

“Nilikuambia Ethan, hii vita si ndog….”

“Nyamaza nguruwe wewe”

Nilizungumza huku niligeuza gari hili kwa kasi sana, likayumba kidogo ila nikafanikiwa kuliweka sawa.

“Tupa hiyo simu ya huyo mzee”

Tuliisikia sauti ya Ethan akizungumza nasi, tukatazamana na Camila usoni mwetu. Nikaanza kujipapasa mifukoni mwangu na kuipata simu ya mzee huyu, nikashusha kioo kidogo na kuitupa dirishani na kuanza safari ya kutokomea sehemu ambayo kwa kweli hatuifahamu na hatujui ni nini hatima yetu na mwanasheria wangu huyu.



“Tunakwenda wapi huku mume wangu?”

Camila alizungumza huku tukiendelea kufwatisha barabara ndogo iliyopo katikati ya msitu huu wenye miti mirefu kwenda juu na iliyo fungamana sana.

“Twende tu mke wangu, hatuwezi kurudi mjini kwa hali hii”

Meneja akakurupuka na kujikuta nikitazama nyuma alipo kaa. Nikamuona Ethan akiwa amekaa pembeni yake.

“Unaniogopa ehee?”

Ethan alizungumza huku akimshika meneja shati lake. Ethan akaniomba nisimamishe gari na nikafanya hivyo. Kwa ishara akaniomba nishuke kwenye gari ili tuweze kzungumza.

“Muangualie huyu”

Nilizungumza huku nikimtazama Camila, akanijibu kwa kutingisha kichwa huku akiwa ameishika bastola yake vizuri. Nikafunga mlango na tukazunguka nyuma ya gari hili.

“Hali ya usalama wenu sio nzuri fariki yangu. Hali ni mbaya na munawindwa kuuwawa”

Ethan alizungumza kwa sauti ya upole sana

“Duuu na inakuwaje watu wa serikalini ndio wanahitaji kutuangamiza?”

“Raisi wa sasa hivi haitaji kuachia madaraka kwenye chama cha baba yako mkwe. Kumbuka kwamba huyu raisi chama chake ndio hicho anacho gombania huyo mke wa mwanasheria wake. Wewe kwa kumpa msaada wa kipesa wa asilimia hamsini, umewafanya wajenge uadui mkubwa sana. Hivyo wakiwaua wewe na Camila basi baba yake atajitoa kwenye kinyang’anyiro cha kugombani uraisi”

“Hii taarifa inabidi Camila aweze kuifahamu”

“Sawa”

Nikarudi upande wa siti ya Camila, nikamuomba ashuke kwenye gari huku akichomoa funguo za gari hili na tukaifunga milango. Tukasimama nyuma ya gari hili huku tukimtazama Ethan.

“Shemeji kuna swala hapa nahitai kukueleza, nilianza kumueleza Ethan kidogo akaona sio mbaya akakushirikisha na wewe”

“Swala gani?”

“Vita ambayo mupo nayo hivi sasa imeanzia serikalini. Lengo lao ni kuwaua nyinyi wawili ili kuhakikisha kwamba baba yenu anatoka kwenye kinyang’anyiro cha uchaguzi wa raisi”

“Ohoo Mungu wangu, kwa hiyo haya yanayo tokea hivi sasa ni kwasababu ya raisi huyu wa sasa?”

“Ndio”

“Sasa tutafanyaje jamani”

“Popote ambapo mutakuwa ndani ya hii nchi ni lazima muta uwawa kwa maana adui yetu anakuja kwa sura nyingi, mara wanajeshi mara hivi, hivyo hata mimi japo nina uwezo mkubwa, ila wananizidi akili sana na laiti ninekuwa mbali nanyi hawa wanejeshi wangewau”

Nikashusha pumzi huku nikimtazama Ethan.

“Nina rafiki yangu mmoja yupo nchini Tanzania. Nitawasiliana naye kwa sasa ili aweze kuwasaidia kuwaficha huko. Naamini kwamba mashambulizi ya kumuangusha huyu mama kutoka madarakani itaanzia huko huko Tanzania sawa”

“Sawa shemeji ila uchaguzi umebakisha siku ishirini na hivi sasa baba tupo kwenye kampeni kweli si wanaweza kumdhuru”

“Hadi kumfikia baba yako ni kazi ngumu sana na ukumbuke kwamba baba yako anasaidiwa na babu yako ambaye naye alikuwa ni raisi wa hii nchi. Hivyo bado kuna nguvu ambayo aimeicha ndani ya serikali”

“Sawa nimekuelewa shemeji”

Ethan akatoa simu yake na kusogea pembeni.

“Sasa mume wangu kama tukielekea Tanzania, itakuwaje mama na dada yako?”

“Nina imani atawalinda kama anavyo tulinda nasi”

“Kweli?”

“Ndio”

Ethan mara baada ya kumaliza kuzungumza na simu akarejea sehemu tulipo.

“Nimesha zungumza naye. Mutaondoka hapa na helicopter hadi nchini Ufaransa. Kuanzia hapo mutaiza safari ya kuelekea nchini Tanzania na huko mutapokelewa na mwana dada huyo”

“Sawa, sasa dada yangu na mama nina waacha huku itakuwaje rafiki yangu?”

“Nitakuwa nao pamoja na nimeweza kuweka hali ya wao kusahulika, hakuna adui ambaye anaweza kuwakumbuka hata mmoja”

“Ahaa, sawa.”

“Ila nitahitaji kuzungumza na mama pamoja na baba ili tuwatoe wasiwasi?”

“Kwa sasa si rahisi na salama kuzungumza nao. Mutazungumza nao kipindi mukifika nchini Tanzani, sawa”

“Sawa”

“Ingieni kwenye gari, sasa hivi nitawaendesha”

Nikamkabibidhi Ethan funguo, kisha mimi nikapanda siti ya nyuma na kukaa na mwanasheria huku Ethan na Camila wakikaa siti ya mbele.

Safari ikaendelea huku tukizidi kukatiza kwenye msitu huu. Mwanasheria mwili wake unamtetemeka kila anapo mtazama Ethan mwenzangu.

“Yaani sikuamini kama wewe unaweza kuja kuwa mtu ambye unaweza kuja kuniharibia maisha yangu na nimekuwa mkimbizi wa kukimbia kimbia katika nchi ambayo nimekuwa toka nilipo kuwa mtoto mdogo”

“Haya yote nimefnya kwa shinikizo, sio mimi, laiti kama ningekuwa ni mimi nisinge fanya hivi”

“Hiyo sio pointi ya kujitetea”

“Ethan huyo nitabaki naye mimi hapa Ujerumani”

“Sawa nashukuru, ila hakikisha anakuwa hai hadi pale anapo mshuhudia mke wake anavyo anaguka na ikiwezekana anakwenda jela kwa kosa hili”

“Sawa”

Tukafika kwenye moja ya kiwanja kidogo ambacho kimezungukwa na miti. Tukakuta helicopter moja ya kifahari ikiwa katika eneo hili. Tukashuka ndani ya gari na kumuacha mwanasheria peke yake.

“Huyu mzee anatawapeleka hadi Ufaransa, mutapanda ndege na maelezo yote nimemueleza na tutawasiliana mukiwa ndani ya ndege”

“Sawa”

“Shem ni nani ambaye atatupokea huko?”

“Ohoo usijali shemeji, mukiwa kwenye ndege mutakabidhiwa kila kitu chenye melezo sawa”

“Sawa nashukuru shemeji yangu, ninaweza kukumbatia?”

Macho yakanitoka kidogo kwa ombi hilo la Camila kwa Ethan.

“Acha wivu. Unaweza kunikumbatia”

Ethan akapanua mikono yake kidogo na Camila akamkumbatia kwa nguvu sana.

“Imetosha sasa, kukumbatiana gani huko”

“Haahaaa haya”

Ethan alizungumza huku akimuachia Camila taratibu. Tukaanza kutembea na Ethan hadi kwenye helicopter hii. Tukakuna na mzee mmoja wa kifaransa kwenye ndefu nyingi nyeupe.

“Anaitwa mzee Fransico. Mzee Fransico huyu ni Ethan wajina wangu na huyu ni Camila ni mpenzi wake”

“Nashukuru kwa kuwafahamu”

“Karibuni sana nimewajia na nguo za kubadilisha”

“Tunashukuru”

“Munaweza kuingia ndani ya helicopter mukabadilishia humo humo ndani”

“Sawa”

Mimi na Camila tukaingia ndani ya helicopter hii, tukakuta nguo kadhaa, nikavaa suti mija nyeusi yenye shati jeupe, huku Camila naye akivaa gauni moja refu la rangi ya nyeupe ila ina vimweko mweko ya dhahabu. Camila akaziweka nywele zake vizuri huku akivaa miwani moja nzuri ambayo kwa asilimia kubwa imebadilisha muonekano wake.

“Tayari”

Nilizungumza mara baada ya kufungua mlango wa helicopter hii.

“Ohoo umependeza sana wajina”

“Nashukuru ndugu yangu”

“Sawa, hati za kusafiria zote zipo tayari. Mzee atawakabidhi mukifika uwanja wa ndege”

“Poa”

Mzee Fransico akaingia kwenye helicopter hii upande wa rubani. Taratibu akawasha helicopter hii na tukaanza kuondoka katika eneo hili huku tukimpingia mkono Ethan ambaye tukamshuhudia akiingia kwenye gari na kuondoka eneo hili. Safari ya kuondoka nchini hapa Ujerumani ikaanza huku Camila akionekana kujawa na mawazo mengi sana kichwani mwake.

“Baby mbona una mawazo?”

“Namfikiria baba yangu, naondoka nchini kwangu pasipo hata kutegeme kama kweli ninaondoka muda huu”

“Ni kweli mke wangu, ila hili swala litakwisha nina imani kwamba baba akiingai madarakani kila jambo linaweza kwenda vizuri naamini atakuwa na nguvu ya kupigania hili jambo”

“Ni kweli ila nina ogopa sana”

“Usijali nipo karibu nawe”

Safari ya kuelekea nchini Ujerumani ikatuchukua masaa kadhaa hadi kufika katika kiwanja cha Paris Orl. Tukashuka kwenye helicopter ikiwa ni majira ya saa moja kasoro usiku, tukainagi kwenye ndege ya kukodi ambayo ni private jet.

“Ndani ya ndege kuna simu mbili na zina maelezo ya nani atawapokea mukifika nchini Tanzania. Hii ni card ya benk ambayo inaweza kutoa pesa katika nchi yoyote duniani. Ni Gold Master Card”

Mzee Fransico alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.

“Nashukuru mzee”

“Ndani ya ndege kuna kila aina ya huduma ambayo mutahitaji na marubani wetu ni wawili. Mr Cosovo na Mis Anna.

“Tunashukuru kwa msaada wenu”

“Ndani ya akaunti kuna kiasi cha dola milioni tano za Kimarekani, hakikisheni kwamba munaitunza vizuri”

“Asante”

Tukaagana na mzee Fransico kisha tukaingia kwenye ndege hii ambayo abiri ni sisi wawili. Tukaa kwenye siti mbili nzuri, tukajifunga mikanda na taratibu ndege hii ikaanza kuondoka kwenye uwanja huu.

“Nikupe matunda?”

“Ndio mke wangu”

Camila alizungumza huku akiwa amefungua friji ndogo iliyopo pembeni yake. Akatoa matunda mawili aina ya Apple.

“Sikutarajia kurudi nchini Tanzania leo”

“Ndio tunarudi mum wangu”

“Baada ya miaka kumi na mbili sasa nina rudi nchini kwangu”

“Kweli”

“Ndio, hembu naomba simu hapo nisome maelezo ya mpokeaji”

Camila akanikabidhi simu moja, nikaiwasha na kukutana na melezo ya jinsi ya kuifungua simu hii. Nikakutana na maelezo ya jinsi gani ninaweza kuifungua simu hii. Nikaanza kukutana na maelekezo ya kuifungua simu hii. Nikakuta picha ya msichana mmoja ambaye anaitwa Jojo Dany. Ni msichana mmoja mzuri na anaye vutia kwenye macho ya mwanaume.

“Mbona unashangaa sana”

“Huyu ndio msichana ambaye tunakwenda kukutana naye”

Nilizungumza huku nikimgeuzia Camila simu hii niliyo ishika.

“Sawa”

Camila aliitikia kinyonge.

“Ethan nahitaji kuzungumza na baba yangu”

“Sasa hivi?”

“Ndio mume wangu nahitaji kuzungumza naye”

Tukaitazama simu hii niliyo ishika, kisha nikamkabidhi Camila na akaingiza namba ya mkononi ya baba yake.

“Vipi simu inaita?”

“Ndio”

“Halo baba”

“Ohoo asante Mungu kwa kuisikia sauti yako”

“Nipo salama baba yangu, nina mshukuru Mungu, nipo kwenye ndege hivi sasa nina eleeka nchini Tanzania”

“Tutazungumza mambo mengi baba nikifika nchini humo”

“Nipo na Ethan, huu hapa zungumza naye”

“Sawa”

Camila akanikabidhi simu huku usoni mwake akiwa amejawa na batasamu kidogo. Nikaipokea simu hii na kuiweka sikioni mwangu.

“Ndio mzee”

“Nashukuru kwa kuendelea kumlinda mwanangu, ila ninakuomba huko Tanzania munapo kwenda uhakikishe kwamba anakuwa salama”

“Nashukuru baba, ila nina imani kwamba unaelewa ni jambo gani ambalo linaendelea?”

“Ndio kuna kijana amenifwata kama masaa manne yaliyo pita na amenieleza kwa kila kila kile kinacho endelea kwa sasa”

“Sawa baba, nashukuru kwa kulifahamu, ila ninacho kuomba kuanzia hivi sasa jilinde, nahitaji uingie ikulu. Ukiingia ikuli tutakuwa tayari kurudi nchini Ujerumani”

“Sawa nitahakikisha kwamba ninaichukua nchi na maadui zangu wote watakwenda kulipa kwa hili jambo ambalo wamelifanya.”

“Sawa sawa”

“Ila kuna kitu kimoja ninaomba unisaidie baba mke”

“Kitu gani hicho mwanangu?”


“Nakuomba unahakikishie kwamba utashinda uchaguzi mkuu”

Nikasikia mihemo ya kushusha pumzi ya baba Camila, huku ukimya wa sekunde kadhaa ukiwa umetawala.

“Nitashinda japo kuna changamoto nyingi sana mwanangu”

“Ninakuombea baba yangu”

“Sawa, niwatakie safari njema na mukifika nchini Tanzania ninaomba muweze kunifahamisha”

“Sawa baba”

Nikamrudishia Camila simu na akaendelea kuzungumza na baba yake. Safari hii ikatugarimu siku moja ambayo ni zaidi ya msaa ishirini na nne. Tukafika nchini Tanzania majira ya saa sita mchana, kwa bahati nzuri tukamkuta mwenyeji wetu akitusubiria eneo ambayo ndege imetua.

“Karibuni sana Tanzania”

Dada huyu ambaye anaitwa Jojo kama vile tulivyo soma maelezo yake, alizungumza huku akionekana kuwa na furaha kubwa sana.

“Tunashukuru”

Tukapeana mikono kisha tukaanza kuelekea kwenye maegesho ya magari. Baadhi ya watu walijitahidi kunikazia macho nikiamini kwamba watakuwa wanajiuliza maswali mengi sana ya kunifananisha mimi na Ethan wanaye muona kwenye vyombo vya habari au kwenye mitandao ya kijamii. Tukaingia kwenye gari ya Chervolet Captival Extrem na kuondoka katika uwanja huu wa ndege.

Kumbukumbu zangu kuhusiana na safari yangu ya kwanza kundoka nchini Tanzania, ikaanza kurejea kichwani mwangu taratibu. Nikaanza kutazama majengo ya karibu na huu uwanja wa ndege ambao kwa namna moja ama nyingine yameongezeka, kwani kipindi nilipo kuwa ninaondoka nchini Tanzania hayakuwa kama hivi.

“Mbona unashangaa sana Ethan?”

Jojo Dany aliniuliza huku akinitazama.

“Ninakumbuka mambo mengi sana”

“Mambo gani hayo?”

“Siku nilipo kuwa ninaondoka nchini Tanzania, hapakuwa na majengo kama haya”

“Ohoo, ni kweli, nchi imezidi kubadilika hususani hapa jijini Dar es Salaam”

“Ila nilicho kipende kwenye nchi hii ni joto jamani.”

Camila alizungumza na kutufanya tushangae kidogo.

“Joto”

“Ndio. Ujerumani hali ya baridi kwa kipindi chote cha mwaka, inakera kwa kweli. Tumekuwa ni watu wa kuva amakoti tu”

“Haahaa, basi huko tunapo elekea kuna baridi kiasi”

“Ila si kama ya Ujerumani?”

“Hapana huko ni ya kawaida sana, nina imani mutauipenda”

“Sawa”

Jojo akazidi kuendesha gari hili, tukafika kwenye moja ya motel ndogo na tukapata chakula cha mchana kisha tukaendelea na safari yetu. Hadi majira ya saa kumi na mbili jioni, tukaanza kukatiza kwenye msitu mmoja mkubwa ambao kidogo ukaanza kutupa mashaka.

“Musiogope, huku ni sehemu salama ambayo munaweza kuishi kwa amani kwa kipindi chote”

“Mbona ni msituni sana dada Jojo?”

“Nyumba salama siku zote ni lazima ziwe katika maeneo kama haya. Hamuwezi kukaa mjini, kumbukeni kwamba hamumjui adui yenu atawavamia kwa namna gani”

Maneno ya dada Jojo kidogo yakatufariji na kupunguza wasiwasi mwingi tulio nao. Majira ya saa mbili usiku tukafika kwenye moja ya nyumba kubwa ambayo taa zake za nje hazina mwanga mkali sana. Jojo akaanza kushuka kwenye gari kisha nasi tukafwata huku nikiwa nimeshika Camila mkono. Tukamkuta mwanaume mmoja mrefu kiasi huku mwili wake ukiwa umejengeka kwa mazoezi.

“Karibuni sana”

Mwanaume huyu alizungumza huku akitusalimia kwa kunyoosha mkono wake wa kulia. Nikawa wa kwanza kuupokea mkono wake huo ambao hakika ni mgumu kiasi. Akasalimiana na Camila kisha tukakaribishwa ndani katika nyumba hii. Tukamkuta kijana mmoja akiwa ameketi sebleni huku uso wake ukiwa na majeraha kiasi.

“Karibuni sana. Huyu ni baba yangu anaitwa Dany. Huyu ni mdogo wangu anaitwa Randy”

“Tunashukuru kuwafahamu”

“Baba, Randy, hawa ni Ethan na Camila tutakuwa nao hapa kwa kipindi cha mwezi mmoja hivi”

“Karibuni sana. Ethan mimi ni mfwatiliaji wa mpira wako”

“Nashukuru sana Dany”

Tukakaribishwa mezani na tukapata chakila cha usiku huku kijana huyu mara kwa mara macho yake yananitazama jambo ambalo kidogo nikatamani kumuuliza ni kwa nini ananitazama sana ila nikashindwa kutoka na watu waliomo hapa sebleni.

“Ethan una mke mzuri sana, hakikisha kwamba una mlinda”

“Nashukuru sana”

“Ila kuna jambo moja nahitaji kuanzia kesho mujumuike nasi?”

“Jambo gani?”

“Nilazima muweze kujilinda wenyewe, musitegemee sana ulinzi wa watu ambao wamefundishwa vyuoni na mwisho munawapoteza bure”

Maneno ya Dany kidogo yakatufanya tutazamane na Camila usoni mwetu.

“Musiogope, ni mazoezi ya kawaida sana. Najua Camila baba yako atashinda kiti cha uraisi na wewe ulinzi utaongezewa, sasa inabidi ujipange vizuri”

“Sawa Dany nitashukuru”

Tukamaliza kupata chakula hichi cha usiku kisha Jojo akatupelekea kwenye chumba chetu ambacho tutalala kwa siku zote tutakazo kuwepo hapa.

“Vipi umeridhika kwa hayo mazoezi?”

Nilizugumza huku nikimtazama Camila usoni mwake.

“Mimi nipi tayari, kwa hizi ngija ngija tunazo kutana nazo hakika sina hata hamu kwa kweli. Laiti kama tungekuwa vizuri kwenye swala zima la kupamba, wala tusinge kuwepo hapa sasa hivi”

Camila lizungumza huku akinishika kiunoni mwangu, tukatazamana kwa sekunde kadhaa, kisha mkono wangu wa kulia nikaanza kuushusha hadi kwenye makalio yake na nikaanza kuyaminya minya taratibu.

“Ethan mume wangu nimechoka”

Camila alizungumza huku akijitoa mikononi mwangu. Akaanza kuvua nguo zake, akabakiwa na chupi pamoja na sidiiria kisha akaingai bafuni. Nikakichuguza chumba hichi kwa umakini, nilipo hakikisha kwamba kuna usalama wa kutosha, nami nikavua nguo na kuingia bafuni. Tukaoga kwa pamoja na kurudi kitandani na kulaa.

Saa kumi na mbili alafajiri mlango wetu ukagongwa, tukaisikia sauti ya Jojo akituhamsisha tuamke na tuanze mazoezi. Nikawa wa kwanza kuamka kitandani na kuvaa boksa yangu. Nikatembea hadi mlangoni nikafungua na kumkuta dada Jojo akiwa ameshika nguo za mazoezi. Akanikabidhi nguo hizi kisha akaelekea kwenye chumba kingine na kugonga.

“Ohoo Mungu wangu”

Nilizungumza huku nikiwa ninapiga miyayo mingi sana. Nikajitupa kitandani ambapo Camila bado amelala. Kabla hata usingizi huu wa asubuhi haujanipitia, nikasikia mlango ukigongwa kwa nguvu na kutufanya wote tukurupuke kitadani.

“Muna dakika moja ya kutoka nje”

Tuliisikia sauti nzito ya Dany na kunifanya nianze kuzichambua hizi nguo za mazoezi.

“Jamani haya ni mateso sasa”

Camila alizungumza huku akipiga miyayo mingi sana.

“Tungekataa jana haya wala yasinge tukuta”

“Kwani mimi nilijua mambo yenyewe yanaweza kuwa hivi jamani?”

“Ndio hivyo mke wangu, tukafanye tu. Tukiona mambo magumu leo, tunaomba tuache tu kwani lazima”

“Mmmmm kumbuka tupo ugenini na huku hayupo Ethan wala mtu ambaye atatusaidia hata tukiwa na shida”

“Haaah! Tutajua mbele ya safari bwana”

Nilizungumza huku nikianza kuvaa nguo taratibu, Camila naye akavaa nguo zake.

“Sasa tunakwenda kufanya mazoezi peku?”

“Sijui mimi”

Camila alinijibu huku akiw aamenuna kutokana na uchovu huu wa asubuhi. Tukatoka chumbani hapa na kuanza kutembea kwenye kordo hii ndefu. Tukashuka ngazi na kuwakuta Dany, Camila na Randy sebleni.

“Viatu jamani”

Nilizungumza huk nikiwatazama. Dany kwa ishara akatuonyesha kwa ishara miguu yake ambayo haina hata soksi, akafungua mlango wa sebleni na tukaanza kutoka.

“Tunakimbia hivi jamani?”

Niliuliza huku nikimuona Dany akianza kukimbia kwenye barabara hii ndefu tuliyo jia. Hakuna ambaye alinijibu zaidi ya watu wote kuanza kufwata nyuma. Camila naye hakunijibu zaidi ya kunitazama tu, tukaanza kukimbia kwenye mchanga huu ambao umejaa vijiwe jiwe vidogo ambavyo mara kwa mara mimi na Camila vilituchoma na ilitulazimu kutulia kidogo ili kutoa vijiwe hivyo.

“Oohoo jamani tutakufa”

Nililalama huku nikiandelea kuwafwata nyuma kwa kukimbia.

“Jikaze bwana mume wangu, je ungeenda jeshi ingekuwaje?”

“Bora ujue upo jeshi mke wangu kuliko huku”

“Acha hizo una kera bwana, kumbuka wewe ni mchazaji mzuri wa mpira”

“Kuna tofauti ya uchezaji na mazoezi haya”

“Sitaki bwana kusikia maneno yako”

Camila alizungumza kwa ukali huku akionekana dhairi kwamba ana jikaza.

“Msitu huu una wanyawa wote wakali, hakikisheni kwamba tunapo kimbia munakuwa karibu nasi, tunaingia msituni sasa”

Dany alizungumza huku akiwa amepunguza kasi ya kikimbia na kuwa sambamba nasi tunao jikongoja

“Wa….wany….a..nyama waka…li!!?”

Niliulliza kwa wasiwasi mwingi sana huku macho yakiwa yamenitoka.

“Tazama kule”

Dany alizungumza huku akinyoosha mkono wake wa kulia, nikahisi kama roho inanitoka kwani kwenye moja ya mti kuna joka moja kubwa sana ambalo toka kuzaliwa kwangu leo hii ndio nimeweza kuliona. Woga ukanifanya niongeze mwendo wa kukimbia na kuwa sawa na Jojo huku Camila na Dany wakitufwata kwa nyuma na Randy yupo hatua chache pembeni yetu.

“Vipi unaogopa?”

“Sana”

“Usiogoepe, hakuna mnyama anaye weza kuwashambulia mukiwa nasi. Huwa tumewafundisha mbinu ya kutusikiliza na kutii kile ambacho tunakihitaji wakifwate.”

“Kivipi?”

“Ulisha wahi kumuona mbwa?”

“Ndio”

“Mbwa ukimfundisha baadhi ya vitu huwa ana kisikiliza kama ni bwana wake unaye muongoza, ni sawa sawa na hawa wanyama”

Mapigo ya moyo yakazidi kutuenda kasi sana mara baara ya kuonda kundi la Simba kama watano wakiwa wamelala mbele katika barabara tunayo ipita. Jojo akawafukuza Simba hawa kwa ishara na wakatupisha na kuendelea na mazoezi yetu.

Hadi tunamaliza mazoezi haya ya kukimbia, hakika kama sijafa leo kwa woga basi sinto kufa maisha yangu yote kwa woga, labda kifo changu kisababishwe na jambo jengine, kwani leo nimeona wanyama wakila aina na wengine wanatisha ila hapakuwa na mnyama hata mmoja ambaye ametudhuru.

“Hahahaa haki ya Mungu napenda sana kuishi huku”

Maneno ya Camila aliyo yazungumza huku akiwa amesimama pembeni yangu, yakanifanya nimgeukie huku nikiwa nimejawa na mshangao mkubwa sana.

“Nini?”

“Napenda kuishi huku, yaani Ujerumani hakuna wanyama kama hawa nilio waona leo”

“Hivi hujui kama wale wanyama wanaua, wakikung’ata eheee?”

“Najua, ila nitahakikisha kabla ya kuondoka nimesha jifunza jinsi ya kuishi nao. Haki ya Mungu ninapenda wanayama mimi jamani ohoo”

Nikajikuta nikiondoka eneo alilo simama Camila na kumfanya acheke sana.

“Mbona mpenzi wako anakucheka sana”

Jojo aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.

“Ahaa ni mambo yake ya wanyama wanyama. Ananikera sana sipendi kabisa wanyama”

“Kwa nini uwapendi, ikiwa wao ndio walinzi wetu hapa msituni. Hakuna binadamu mwenye nia mbaya ambaye anaweza kukatiza hapa”

“Mmmm mimi sijaumbwa kwa kweli kuwapenda hao wanyama”

“Hahaa usijali kila jambo litakuwa sawa”

Tukaingia katika awamu ya pili ya mazoezi ya taikondo. Mazoezi haya hakika ni magumu kuliko hata kukimbia katika msitu wa eneo hili. Zaidi ya masaa mawili saa Jojo na Danya wakawa wanatufundisha mazoezi haya ambayo hakika hadi tunamaliza wote watatu viungo vyetu vimeorojeka kwa kuchoka na kuapa majera kadhaa yaliyo tokana na kukosa umakini.

“Camila”

Nilimuita Camila huku tukiwa ndani ya chumba chetu, kwa maumivu niliyo nayo nikajikuta hata nikishindwa kulala kitandani.

“Mmmmm”

“Mimi nahitaji kutoroka, siwezi kuendelea kukaa hapa”

“Mmmm…….”

“Ndio nahitaji kutoroka, maisha gani haya ya mateso naomba ujumuike nami mke wangu na tutoroke wote”

“Umewashaua wale Simba na wanayama wengine humu msituni ehee?”



Nikaka kimya huku nikimtazama Camila usoni mwake. Ukiachilia Simba na wanyama wengine ambao wapo katika msitu huu, ila kusema kweli hatufahamu ni wapi tulipo.

“Mume wangu wewe ni mwanaume, hakuna haja ya kukimbia mazoezi, tena ikiwa wewe ni mchezaji mpira, tena mchezaji ambaye dunia kwa sasa ina kutazama. Tafadhali nina kuomba mume wangu tuwe wavumilivu, siku na muda wa kuondoka utakapo fika basi tutaondoka”

“Nimekuja huku ili niwe mtalii wa kujua mambo mbalimbali ila si kuja kuwa mwanajeshi?”

“Jamani mume wangu, umesahau tabu na ngija ngija tulizo pata na kama ingekuwa si Ethan, haki ya Mungu nina apia leo sijui tungekuwa wapi?”

“Kwa hiyo unahitaji tuendelee kuwa wanajeshi wa hiyari ehee?”

“Sio wanajeshi wa hiyari mume wangu ila tunajilinda sisi wenyewe bwana”

“Sawa”

“Usiseme sawa kinyonge jamani”

Camila alizungumza huku akinikumbatia, ila kwa maumivu makali ya mwilini mwangu nikajikuta nikimsogeza pembeni kidogo.

“Nini”

“Mwili wote unauma bwana mke wangu”

“Hahaa hata nikikupa sasa hivi utashindwa?”

“Ndio”

“Hahaa kweli umeshindwa mume wangu”

Camila alizungumza huku akicheka sana jambo lililo nifanya nimtazame kwa macho ya masikitiko. Usingizi ukanipitia taratibu, alfajiri na mapema kama kawaida tukaamshwa ili kufanya mazoezi kama kawaida.

“Yule jamaa yupo wapi?”

Nilimuuliza Jojo mara baaya ya kujikuta tupo wanne tu katika uwanaja wa mazoezi.

“Yupo kazini”

“Kazini kivipi?”

“Ni mfanyakazi wa moja ya benk katika hii nchi, ila siku mbili hivi atarejea”

“Sawa”

Tukaendelea kufanya mazoezi japo siku ya leo hayakuwa m agumu sana. Baada ya masaa mawili ya mazoezi tukaruhusiwa kuendelea kwa mamabo mengine binafsi.

“Ninaweza kuzungumza na baba yangu?”

“Kwa kutumia video call au?”

“Kama itawezekana”

“Sawa twendeni huku”

Jojo alizungumza huku tukianza kumfwata kwa nyuma. Tukaingia kwenye moja ya chumba kama ofisi, tukakuta moja ya computer kubwa kiasi. Akaiwasha na akaanza kufanya mawasiliano na baba Camila, baada ya muda kidogo akapokea msaidizi wa baba Camila.

“Hei Jonson”

Camila alizungumza huku akiwa amejawa na furaha kubwa sana usoni mwake.

“Hei Camila vipi upo wapi?”

“Mmmm, nipo mbali kidogo. Ninaweza kumpata baba”

“Yupo kwenye kampeni ana hutubia kama upo karibu unaweza kuwasha televishion kumtazama jinsi anavyo hutubia”

“Ohoo inachukua muda gani?”

“Kama dakika ishirini hivi”

“Ninaweza kumsubiri nina hitaji kuzungumza naye sana”

“Sawa, akitoka basi nitamfahamisha na atawasiliana nawe”

“Sawa sawa”

Tukaendelea kukaa ndani ya ofisi hii kwa zaidi ya nusu saa, ndipo baba Camila akapatikana.

“Habari zenu vijana wangu”

Baba Camila alizungumza huku akiwa amejawa na furaha. Jojo akatoka ofisi humu na kutuacha sisi wawili.

“Salama tu baba, vipi kampeni zako zinaendaje?”

“Zinakwenda vizuri na kupotea kwenu kunazidi kuwapa wananchi hasira ya kuhitaji mimi niiingie madarakani ili niweze kukomesha utekaji ambao unaendelea”

“Mmmmm watu wana masikitiko?”

“Yaa wana masikitiko makubwa sana”

“Muheshimiwa samahani kidogo kwa kuwaingilia mazungumzo yenu”

“Hakuna shida Ethan, zungumza tu”

“Vipi familia yangua umeweza kuitembelea au kuwajulia hali?”

“Ndio nilizunguza na Mery pamoja na bi Jane Klopp na wapo salama na niliwaeleza juu ya usalama wenu”

“Nashukuru sana baba”

“Vipi Ethan mbona uso wako kama una kovu kidogo hapo usoni mwako”

“Baba huku tulipo yaani ni zaidi ya jeshini”

“Jeshini”

“Hapana baba Ethan ni uoga wake tu baba”

“Hapana baba yaani huku tunapewa mafunzo makali kiasi cha kujikuta ninapachukia huku sana”

“Baba, mume wangu na umahiri wake wote uwanjani ila anaogopa sana. Baba niamini tupo sehemu salama, naamini tukirudi tutakuwa fiti zaidi ya fiti”

Nikamaki nikimtazama Camila kwa macho ya mshangao, tukamaliza kuzunumza na baba yake kisha tukatoka ofisini humu. Tukakuta Dany aiwa amesha kifungua kinywa. Akatukaribisha mezani na tukaanza kupata kifunga kinywa.

“Leo jiandaeni tunakwenda kutembea”

“Wapi?”

Niliuliza kwa shahuku nikimtazama Dany usoni mwake.

“Nitawaambia baadaye ila mujiweke tayari kwa safari”

“Sawa muheshimiwa”

Tukamaliza kupata kifungua kinywa na kurudi chumbani kwetu. Camila akaanza kuvua nguo zake huku akiwa amenipa mgongo. Jinsi mwili wake ulivyo jengeka vizuri nikajikuta nikijawa na msisimko mkubwa sana wa kimahaba. Taratibu nikaanza kumsogelea kisha kwa mkono wangu wa kulia nikakishika kiuno chake taratibu sana. Camila taratibu akajigeuza na kifua chake chenye chuchu zilizo simama vizuri zikanigusa vizuri kifuani mwangu. Hisia za kimapenzi zikazidi kutawala kati yetu na kujikuta tukizama kwenye dibwi zito la mapenzi. Mpute mpute wa mtanange huu ulizidi kuwa mkali kiasi kwamba kila mtu akajikuta akitoa miguno ambayo hatukujali kama tupo ugenini au laa.

***

Tukakapewa nguo za kuondoka eneo hili kuelekea kwenye safari ambayo Dany alituahidi kwamba tunaweza kuondoka. Tulipo hakikisha kwamba tumemaliza kujianda safari ya kuondoka aneo hili ikaanza.

“Tunaelekea wapi?”

“Kuna jambo moja nahitaji kulifanya kwa ajili ya kipaji chako”

“Mmmm”

“Camila mbona unaguna?”

“Kama tunakwenda kwenye uwanja wa mpira nahisi ni jambo la hatari sana”

“Kwa nini?”

“Maadui zetu wanatuwinda”

“Mukiwa nasi hakuna adui yoote ambaye atawadhuru”

Jojo alitujibu huku akitugeukia.

“Kivipi?”

“Musijali nyinyi kuweni na amani tu”

Safari hii ikatugarimu saa moja na nusu hivi, tukafika kwenye moja ya mji mmoja wenye milima mingi na ulio jengeka vizuri kiasi.

“Hapa ni wapi?”

“Hili eneo linaitwa Lushoto, kuna timu ya taifa chini ya miaka kumi na nane wamekuja kuweka kambi hapa kijiandaa na michuano ya kombe la dunia chini ya vijana wenye umri miaka kumi na nane.”

Dany alizungumza huku akisimamisha gari hili kwenye jengo moja la hoteli.

“Unahitaji mume wangu achezee timu ya taifa ya Tanzania ikiwa ana uraia wa Ujerumani”

“Ethan sio mjerumani ni Mtanzania halisi, baba na mama yake ni Watanzania. Ameishi Ujerumani kwa ajili ya matatizo ya hapa na pale”

Camila akanitazama usoni mwangu huku akiwa na masikitiko kiasi kwani kucheza mpira katika timu ya taifa ya Tanzania, basi sinto weza kucheza tena katika nchi ya Ujerumani na hii pia inaweza kuathiri kampeni za baba Camila kwa maana hata tangazo nililo lifanya la kisiasa linaashiria kwamba mimi ni Mjerumani.

“Dany samahani kidogo naomba tuzungumze”

Nilimuambia Dany huku nikisogea pembeni kidogo huku nikimtzama usoni mwake. Dany bila kujali umri wangu akanifwata sehemu nilipo simama.

“Ndio Ethan”

“Natambua kwamba mimi ni Mtanzania”

“Ndio”

“Ila kichwa changu hakina kumbukumbu yoyote kuhusiana na hii nchi hususani familia yangu. Sasa itawezekaje niweze kuichezea hii nchi ikiwa sijakua nchini hapa?”

“Kukua au kuto kulia katika nchi hii hilo sio tatizo”

“Ila”

“Ila fwata chimbuko la wazazi wako”

“Mimi sina kumbukumbu yoyote juu ya wazazi wangu, nitafwata chimbuko langu kivipi sasa?”

“Huna kumbukumbu za wazazi wako?”

“Ndio”

Jojo akatufwata hapa tulipo simama huku akiwa na sura ya tabasamu.

“Ethan”

“Mmmm”

“Huna kumbukumbu yoyote na wazazi wako?”

“Ndio”

“Unahitaji kufahamu ni kitu gani kilicho wapata?”

“Ndio”

Jojo akanisogelea na kunishika kichwani mwangu, nikahisi ubaridi mkali ambao taratibu katika ufahamu wangu wa akili nikaanza kuona ngurumo za radi huku mvua nyingi ikinyesha. Kumbukumbu zangu zikazidi kusonga mbele na kumuona mzee mmoja akiwa amezungukwa na kundi kubwa la vijana huku wakimshambulia kwa kumpiga kwa magongo pamoja na mateke huku wakihitaji afariki dunia.



Nikamuona mama yangu akiwa amejificha kwenye migomba pamoja nami huku akilia. Radi iliyo piga yenye mwanaga mkubwa, ikanifanya niweze kumuona mwanaume mmoja ambaye baada ya kuiona sura yake nikajikuta nikistuka sana.

“Vipi?”

Dany aliniuliza hukua kinitazama usoni mwangu. Nikashindwa kulijibu swali lake kwani mapigo yangu ya moyo yananienda kasi huku jasho likinimwagika usoni mwangu.

“Kuna nini kinacho endelea hapa”

Camila alizungumza mara baada ya kufika hapa tulupo simama. Nikawatazama watu wote hawa kisha nikaondoka na kuanza kuelekea kwenye gari tulipo liacha.

“Ethan, Ethan”

Camila aliniita, sikuweza kumuita zaidi ya kuzidi kusonga mbele. Nikajaribu kufungua mlango wa gari ila haukufunguka.

“Ethna mume wangu kuna kitu gani kinacho endelea?”

Camila alizungumza huku akinishika mkono.

“Nimemuona”

“Umemuoan nani?”

“Mtu aliye niulia baba na mama yangu”

Camila macho yakamtoka kwa maana hakuamini kama ninaweza kukumbuka vitu hivi kwa muda huu.

“Ni nani?”

“Simfahamu jina lake, ila nimeikumbuka sura yake”

“Ohoo jamani mpenzi wangu, tulia kidogo”

Camila alizungumza huku akinikumbatia mwilini mwangu. Dany na Jojo wakanifwata sehemu hii tulipo simama.

“Ethan umeona nini?”

Jojo aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.

“Nimemuona mtu aliye niulia baba na mama yangu”

“Una uhakika?”

“Ndio”

“Twendeni ndani jamani”

Dany alishauri na kutufanya mimi na Jojo kumtazama. Dany akaanza kuongoza kuelekea ndani, nasi tukaanza kumfwata kwa nyuma. Tukaelekea eneo lenye kiwanja kikubwa cha mpira. Tukakutatimu ya vijana chini ya miaka kumi na nane wakifanya mazoezi katika eneo hili. Baadhi ya watu nao wamejumuika katika kuitazama timu hii. Tukakaa katika moja ya sehemu ambayo tunaweza kuona mazoezi yao vizuri sana.

“Ethan”

“Naam”

“Mtu huyo anafananiaje?”

Nikamtazama Jojo huku nikijaribu kuvuta kumbukumbu yake, kitu kilicho nishangaza, sikuweza kuipata kumbukumbu yake tena.

“Mbona simkumbuki”

“Humkumbuki?”

“Ndio”

“Ngoja”

Jojo alizungumza huku akinishika kichwani mwangu, nikaanza kuoana jinsi mwanaume huyo alivyo toa amri ya sisi kukimbizwa pamoja na mama yangu. Mama akajitahidi kukimbia kwa kuchechemea huku akiniongelesha kwa lugha ya kichaga kwamba tukimbie. Kutokana na utoto wangu nikakimbia hadi kwenye migomba mingi ila nikashindwa kuendelea na kukimbia, nikarudi sehemu alipo mama yangu na kukuta akitaka kubakwa na vijana walio kuwa akitukimbiza. Vijana wawili wakaninyanyua juu juu na kunipeleka hadi kwenye korongo. Kitendo cha kujigonga kichwa changu kwenye jabali nikakurupuka tena huku nikishika kichwa changu upende ambao nilijibamiza kwenye korongo.

“Vipi umeona nini?”

Nikashusha pumzi taratibu huku nikimtazama Jojo usoni mwake.

“Nimeona jinsi mama alivyo kuwa akibakwa na mimi nikapigwa na kusukumia kwenye korongo”

“Hujamuona tena huyo mtu?”

“Hapana”

“Ukimuona picha je utamkumbuka?”

“Nahisi, ila kumuelezea kwamba yupo vipi siwezi kwa kweli”

“Chukua muda wa kutosha ukimkumbuka basi utanifahamisha sawa”

“Sawa”

Camila akanisogelea karibu yangu na kunishika mkono wangu na kukiegemesha kichwa chake karibu yangu.

“Unajisikiaje mume wangu?”

“Sasa nimejitambua mimi ni nani?”

“Kivipi?”

“Jina langu sio Ethan mpenzi wangu”

“Mmmmmm?”

“Yaa jina langu sio Ethan, jina hilo nimepewa ila sio lile nililo pewa na wazazi wangu”

Camila akabaki akiwa na mshangao mkubwa sana huku akinitazama usoni mwangu.

“Jina lako halisi ni lipi?”

“Naitwa LOLE, hilo ndio jina langu katika kabila langu la Kichaga”

“Wachaga ni watu wa wapi?”

“Moshi”

Camila akaka kimya huku akinitazama usoni mwangu akionekana kutafakari haya mambo niliyo mueleza.

“Lole sinto kuita Ethan tena sawa mume wangu?”

“Nashukuru mke wangu”

Nikamkumbatia taratibu Camila, tukaendelea kutazama mazoezi ya wachezaji hawa, japo wana kocha ila yamejaa udhaifu mkubwa sana.

“Natamani nikawaelekeze kidogo mke wangu”

“Mazoezi!?”

“Ndio”

“Ohoo mume wangu wasije wakahitaji kukuchukua, kumbuka mambo yaliyo tutokea Ujerumani”

“Nawaelekeza kidogo, kidogo tu”

“Mmmm haya”

Nikamuachia Camila na kuanza kushuka ngazi na kuelekea uwanjani. Walinzi wanao linda wachezaji hawa wakanizuia kuingia.

“Samahani kuna machache nahitaji kuzungumza na kocha, tafadhali ninaomba munisaidie katikahilo”

Mmlinzi mmoja akanikazia macho sana, kisha baada ya muda kidogo akatabasamu.

“Kama sijakosea wewe ni Ethan Klopp?”

“Yaa ndio mimi”

“Pita pita”

Mlinzi huyo alizungumza kwa furaha kubwa sana na kuwafaya wezake nao wajawe na furaha kwa maana hapo awali hawakuweza kunifahamu. Nikafika katika sehemu walipo simama makocha wawili mmoja akiwa ni kocha wa kizungu. Nikasalimiana nao kwa heshima sana, kwa bahati nzuri wakaweza kunifahamu kwa haraka sana.

“Ohoo Ethan upo Tanzania?”

Kocha huyu wa kizungu alizungumza huku akiwa amejawa na mshangao sana.

“Ndio nina siku ya pili sasa japo nimekuja Tanzania kwa siri sana”

“Ohoo karibu sana yaani nilikuwa ninatamani sana kukuita kwenye kikosi changu ila sikuweza kufahamu ni wapi nitakupata”

“Nimekuja kwenye mapumziko mafupi, ila nitaandoka”

“Oohoo sasa unataka kuniambia kwamba huto kuwepo kwenye fainali zinazo endelea Ujerumani?”

“Yaa sinto kuwepo kwenye kikosi, naamini kama ni mfwatiliaji wa mambo utaweza kugundua ni kitu gani ambacho kimetokea kwenye wiki za hivi karibuni”

“Yaa nafwatilia”

“Ndio maana nipo hapa. Kuna mambo kadhaa ambayo naomba niweze kuwaelekeza timu yako. Nimekaa juu kule nikaona mapungufu kadhaa. Sijui unaweza kunipa nafasi japo dakika kumi na tano nikafundisha vijana wako”

“Kwa nini usiingie ukacheza ndani?”

“Hapana, labda siku nyingine, ila leo nahitaji kutoa maelekezo madogo madogo ili tumu iwe vizuri”

“Sawa darasa ni lako”

Kocha akapiga filimbi na wachezaji wote wakakusanyika sehemu tulipo simama sisi. Nikasalimiana na wachezaji hawa ambao nao wakaonekana kufurahi sana kwangu.

“Mimi ni Mtanzania kama nyinyi tena ni mchaka. Hivyo naomba musiwe na ile hali ya kuhisi labda mimi ni mtu maarufu au nimetokea Ujerumani, hivyo mukajihisi unyonge kwenye mioyo yao. Mimi sifahamu mengi sana kwenye mpira, ila kwa yale machache niliyo nayo, nimeona ni vyema tukabadilisha yote katika yote ni kuweza kuijenga timu yetu si ndio”

“Ndio ndio”

Nikaanza kuwapa mbinu washambuliaji pale wanapo kuwa uwanjani. Nikagawa timu hii mara mbili kisha nikasimama kama refarii. Wakaanza kucheza mpira kama vile nilivyo walekeza, ndani ya dakika kumi thelathini, wakacheza kwa kiwango cha hali ya juu hadi watu hawa walio kuja kushuhudia mazoezi haya wakaanza kushangilia kana kwamba wanatazama mechi ya wapinzani. Kutokana tayari imesha kuwa jioni, nikapiga kipenga cha kumaliza mpira huu. Kila mchezaji akanifwata na kunipa pongezi kwa maelezo mazuri ambayo nimewapa.

“Kwa nini usibaki na sisi ukawa mchezaji?”

Mchezaji mmoja alizungumza huku tukiwa tunatembea kutoka uwanjani hapa.

“Hapana rafiki yangu kila jambo linawakati wake, wakati wangu wa kucheza hapa Tanzania ukifika basi nitacheza”

“Sawa, ila hakika wewe ni kocha bora kwa kweli, yaani huyu mzungu hapa anakula pesa za serikali yaani anatufundisha kawaida sana”

“Ngoja niwaambie kitu kimoja”

“Kitu gani?”

“Siri ya kuwa timu bora sio kocha. Nyinyi wachezaji munatakiwa kuwa upande kati yenu na mujue kwamba nyinyi ni kama familia ya baba mmoja. Mukipambana hakikisheni kwamba munapambana kama familia, musiangalie eti yule ana uwezo au yule hana uwezo. Mukishikamana hakika kocha yeye kazi yake itakuwa ni kusimama tu nje ya uwanja, ila nyinyi mutajua ni nini munafanya”

“Kweli kaka unacho zungumza ni kitu cha kweli kabisa. Unajua tatizo letu sisi huwa tumetolewa kila mtu kwenye timu yake hivyo tukikuatana hapa utakuta huyu anacheza hivi huyu anacheza hivi yaani ni tabu tu?”

“Hiyo sio sababu ya maana. Muna muda gani toka muweke kambi?”

“Leo siku ya tatu?”

“Katika masaa mawili nyuma mulikuwa muna chezaje?”

“Kawaida?”

“Sasa toeni ukawaida, hakikisheni kwamba munacheza kwa kujituma na upendo, acheni kuweka matabaka. Kapteni ni nani?”

“Ni mimi”

“Ohoo kumbe nipo na timu kapteni. Sasa wewe ndio wa kuyafanyia kazi kama vile nilivyo kuelekeza sawa kaka”

“Sawa”

Tukafika sehemu walipo makocha hawa wawili, tukakusanyika kwa pamoja.

“Jamani mumeona mulicho cheza leo. Sasa nataka iwe hivi hivi kwenye mashindano ya kombe la dunia ambayo tunaiendea”

Kocha alizungumza huku akiwa amejawa na furaha sana. Wakanipongeza sana huku wakiniomba kesho niweze kurejea ili nizidi kuungana na makocha hawa katika kuhakikisha tunakinoa kikosi hichi cha vijana.

“Nitazungumza na wenyeji wangu kama wataniruhusu kufika hapa kila siku”

“Kwani wenyeji wako ni kina nani?”

“Wapo kule juu”

Nilizungumza huku nikiwatazama Dany, Jojo na Camila sehemu walipo kaa.

“Sawa naomba uzungumze nao”

“Sawa jamani kwa herini”

Nikaondoka eneo hili huku wachezaji wakiwa wamejawa na furaha kunwa sana. Nikajimuika na wezangu huku nao wakionekana kunisifia hususani Dany. Tukaondoka katika eneo hili na kuelekea katika hoteli nyingine kwa ajili ya chakula cha usiku. Tukaagizia chakula tunacho kihitaji na baada ya muda muhudumu akatuletea chakula hicho. Moyo ukanistuka kwa mara nyingine mara baada ya kumuona mwanaume ambaye ameniuliza wazazi wangu katika taarifa ya habari, akiwa ni miongoni mwa wagombea walio tangaza nia ya kogombania kiti cha uraisi katika nchi hii ya Tanzania.



Nikajikuta nikisimama kwenye kiti nilicho kikalia na kuanza kutembea hadi hadi karibu na tv hii jambo lililo wafanya Camila na watu wengine kushangaa sana. Nikamtazama mwanaume huyu huku kifua changu kikiwa kimejawa na hasira kali sana.

“Ethna”

Nilistuka mara baada ya Camila kunishika begani mwangu. Nikamtazama usoni mwake huku nikishusha pumzi nyingi sana.

“Vipi mume wangu”

“Huyu mwanaume”

“Amefanyaje?”

“Ndio aliye niulia wazazi wangu”

Camila macho yakamtoka huku akijiziba mdomo wake kutoka na an mshanagao mkubwa ulio mpata.

“Kama kweli yupo hapa Tanzania lazima nami nimuue”

“Ethan zungumza kwa sauti ya chini kidogo si unajua kuna watu wengi”

Camila alizungumza huku akinishika mkono na kurudi tulipo kuwa tumekaa.

“Vipi?”

Dany aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.

“Yule mwanaume pale ndio aliye niulia wazazi wangu”

Dany na Jojo wakastuka kidogo huku wakinitazama usoni mwangu.

“Unasema kweli?”

“Sina haja ya kuwaongopea, ninacho kizungumza ni kitu cha ukweli na ninamkumbuka vizuri sana”

Ukimya ukatawala huku Dany na Jojo wakiitazama taarifa hii ya habari. Sikuweza hata kuendelea kupata chakula hichi, nikanyanyuka na kuelekea sehemu ya maegesho ya magari.

‘Fuc* Fuc*”

Nilizungumza huku nikipiga piga tairi la gari tulilo jia.

“Ethan utajiumiza mume wangu usiwe hivyo bwana”

Camila alizungumza huku akinikumbatia kwa nyuma.

“Najua una hasira mume wangu, ila nina kuomba sana mpenzi wangu uwe mvumili, tutahakikisha tunamfungulia mastka na atashtakiwa kwa mujibu wa sheria za nchi hii”

“Nchi hii, unahisi mtu ana nguvu ya kwenda kugombania urahisi, unahisi atastakiwa ehee?”

“Ethna”

“Sio Ethan Camila. Hii sio Ujerumani, huku ni barani Afrika. Bara la watu weusi, hakuna haki, mwenye nguvu ana nguvu na asiye na nguvu hato kuwa na nguvu mke wangu”

Nilizungumza huku nikimwagikwa na mchozi usoni mwangu.

“Sasa mume wangu unahitaji tufanye nini?”

“Nahitaji alipe kwa kila baya alilo lifanya juu ya maisha yangu na wazazi wangu”

“Nitahakikisha mume wangu nina kuwa nawe bega kwa bega kuhakikisha kwamba una fanikiwa katika kazi yako hii ya kulipiza kisasi sawa mume wangu?”

“Nashukuru mke wangu”

Jojo na Camila wakatufwata sehemu tulipo na tukaondoka eneo hili. Ndani ya gari sikuzungumza kitu chochote hadi tukafika nyumbani.

“Ethan nahitaji kuzungumza nawe”

Dany alizungumza huku akishuka kwenye gari, nikaanza kumfwata hadi nyuma ya nyumba hii, akafungua geti kubwa na kuingia ndani ya ukumbi mkubwa sana ambao umejaa vitu vingi, ikiwemo silaha kubwa kubwa ambazo sikuwahi kuziona kwenye maisha yangu.

“Kaa hapo”

Dany aliniambia huku akinionyesha moja ya kiti cha kuzunguka kilichomo pembeni ya meza kubwa. Nikaka kwenye hichi kiti huku naye akizunguka kwenye meza hii na kukaa kwenye kiti kingine. Dany akaminya minya batani ya laptop iliyopo mezani mwake kisha akanigeuzia.

“Ni huyu”

Dany alinionyesha picha ya mzee ambaye ameniulia wazazi wangu. Nikafumba macho kwa sekunde kadhaa kisha nikafumbua na kumtazama tena.

“Ndio ni yeye”

“Anaitwa Poul Mkumbo, kabila lake ni Mnyiramba. Ana uwezo wa asilimia sabini na tano ya kuwa raisi wa nchi hii na ana nguvu katika jamii kwa maana alijitengenezea nafasi ya kugombania uraisi zaidi ya miaka kumi na mbili kwa sasa”

“Nitampataje?”

“Unahitaji kumuua?”

“Nahitaji alipe kwa yale yote ambayo amenitendea kwenye maisha yangu”

“Kulipa kupo kwa aina nyingi, moja ni kumuua je hiyo ya pili una hitaji kumfanya nini?”

“Kwanza nahitaji ngome yak e aliyo ijenga kwa miaka yote hiyo kuiangusha na ninahitaji kurudisha kila kitu alicho kichukua kwa wazazi wangu ana kirudisha”

“Alichukua ni na nini?”

Kumbukumbu zangu zikanirudisha kipindi nipo na wazazi wangu katika shamba letu moja kubwa la migomba. Katika harakati za wazazi wangu kupalilia migomba hii huku nami nikiwa nina cheza cheza pembeni ya moja ya mgomba huku nikichimba chimba chini, nikaona jiwe moja kubwa kiasi likiwa ni tofauti kabisa na mawe ambayo nilisha wahi kuyaona kwenye maisha yangu. Nikamkimbilia baba yangu na kumuonyesha jiwe hili, baba na maam wakaanza kutazama jiwe hili na kuniuliza ni wapi nilipo litoa.

Nikawaonyesha sehemu ambayo tumelitoa jiwe hili, baba akaanza kuchimba katika eneo hili na kuona jiwe jengine linalo fanania na jiwe hili.

“Hii ni dhahabu”

Maneno ya baba niliyakumbuka vizuri sana huku akiwa na furaha kubwa sana huku machozi yakimlenga lenga usoni mwake.

“Eneo hili lina dhahabu, hii ni mali mke wangu tumesha kuwa matajiri”

Baba aliendelea kuzungumza kwa furaha kubwa sana, kutokana hapa shambani si mbali sana na nyumbani, akaniagiza niweze kwenda nyumbani kuleta moja ya kibegi ambacho hukitumia sana pale anapo kwenda mjini kuuza mikungu ya ndizi.

Kumbukumbu zangu zikazidi kusonga mbele hadi pale nilipo fika nyumbani, nikatafuta kibegi hicho, japo ilinichukua muda mwingi sana kuweza kuwapata, ila niliweza kufanikiwa kukiona.

Nilipo rudi shambani, nikamkuta baba pamoja na mzee mmoja ambaye ni rafiki yake huku wakiwa wanachimba eneo hilo ambalo lina mawe haya ya dhabu. Nikakumbuka kibegi hicho kilijaa mawe hayo yanayo ng’aa sana na kururahisha unapo yatazama. Usiku wa siku hii ndipo tulipo vamiwa na kundi la vijana pamoja na mzee huyu bwana Mkumbo na hapo ndipo yalipo kuwa ni matatizo yangu na familia yangu.

“Utajiri wake mkubwa umetokea kwenye mgoni wa dhahabu huko Arusha ana umiliki”

Maneno ya Dany yakanistua sana na akaanza kunionyesha picha nyingine za mgodi mkubwa sana ambao unamilikiwa na bwana Mkumbo jambo ambalo limenifanya nizidi kuchanganyikiwa na kushikwa na hasira sana.

“Huu mgodi upo kwenye eneo ambalo ni mali ya wazazi wangu, ninahitaji kuuchukua”

“Hilo unalo lizungumza sio jambo rahisi sana”

“Nina akili na nina uwezo wa kufanya kila kitu na nitahakikisha kwamba ninafanikiwa”

“Etthan”

“Ninaomba unipatie taarifa zake na mali zake zote anazo zimiliki nitaanza kushuhulika na moja baada ya jingine”

“Unahisi njia hiyo unayo hitaji kuitumia ni sahihi kuweza kupata hizo mali?”

“Ndio”

“Sawa”

“Nitakapo hitaji msaada wako nitakujulisha na kesho nahitaji kwenda jijini Dar es Salaam, naamini huko ndipo nitakapo kwenda kufanya mipango yangu ili iweze kwenda”

“Dar es Salaam?”

“Ndio””

Dany akakaa kwa sekunde kadha kisha akatingisha kichwa ikiwa ni ishara ya kunikubalia kile nilicho muomba. Dany akafungua droo ya hii meza na kutoa moja ya simu na kunikabidhi.

“Utaitumia hii na ina kila aina ya habari za mgombea uraisi bwana Mkumbo. Utazipitia usiku kucha kisha kesho nitapanga safari ya wewe kuelekea jijini Dar es Salaam”

“Sawa”

Nikatoka ndani humu na kurudi chumbani kwangu na kumkuta Camila akiwa amekaa kitandani akinisubiria.

“Vipi kuna kitu gani kinacho endelea?”

“Nahitaji kupambana sasa”

“Kivipi mpenzi wangu?”

Nikaanza kumuelezea Camila juu ya mzee huyu. Nikamueleza na historia nzima ya maisha yangu na ya wazazi wangu, katika umri huu sasa ndipo nilipo weza kufahamu kwamba baba na mama yangu walikuwawa na mzee Poul Mkumbo kwa ajili mgodi wa madini.

“Kesho nitakwenda Dar es Salaam na wewe utabaki hapa sawa”

“Dar es Salaama unakwenda kufanyaje tena mume wangu”

“Nalianzisha hili swala, nitakuhitaji ubaki hapa sawa”

“Ethan hapana, siwezi kukuacha wewe uende peke yako. Kumbuka kwamba hili jambo ni letu wote tafadhali mume wangu”

Camila alizungumza huku machozi yakimlenga lenga usoni mwake.

“Hapana sihitaji nikuweke matatizoni Camila. Kumbuka kwamba hii vita ni yangu, wewe kaa kama silaha yangu ya siri, siwezi kuingia vitani na silaha zangu zote za maangamizi kwa maana mtu ambaye ninakwenda kupambana naye sifahamu ana uwezo gani, sijui ana weza kutumia nguvu gani na kumbuka ninakwenda kumuangusha raisi ambaye anakwenda kuingia madarakani huku nyuma akiwa na dhambi na damu za watu ambao amewapokonya haki zao. Umenielewa?”

Nilizungumza kwa msisitizo na kumfanya Camila kukaa kimya huku akiendelea kumwagikwa na machozi usoni mwake.

“Nakupenda Camila nakuhitaji mke wangu. Ila acha nifanye hii kazi. Nina muda mfupi sana ila nakuomba mpenzi wangu unielewe sawa”

Camila akajibu kwa kutingisha kichwa akimaanisha kwamba amenielewa kile nilicho mueleza.

“Nitakujulisha kila kila kitu ambacho kitakuwa kinaendelea katika katika kazi yangu sawa”

“Nimekuelewa mume wangu”

Tukakumbatiana na Camila kwa nguvu sana huku kila mmoja akiwa amejawa na huzuni pamoja na uchungu mwingi sana. Usiku huu, tukapeana penzi zito kana kwamba hatuto peana tena kwenye maisha yetu ya baadae.

***

Tukaanza safari ya kuelekea jijini Dar es Salaam, tukiwa tumeongozana na Jojo, huku Dany akimsisitizia Jojo aweze kunilinda kwa kila namna. Safari ya kufika jijini Dar es Salaam ikatuchukua takribani masaa saba kwani nakumbuka ni sehemu moja tu ndio tulisimama ili kuweza kupata chakula cha mchana. Tukafika katika hoteli moja ya kifahari yenye hadhi ya nyota tano, Serena Hotel. Nikawasiliana na Camila na kumueleza kwamba tayari nimesha fika jijini Dar es Salaam na akanitakia kila la heri katika kuhakikisha kwamba nina ianzisha vita yangu ambayo haito mwaga damu ila itajaa uchugu na mateso makubwa sana kwa mzee Poul Mkumbo.

“Nakusikiliza Ethan, mpango wako wa kwanza ni upi?”

Camila aliniuliza huku akiwa ameweka nne kwenye sofa alilo kalia ndani ya chumba hichi tulicho fikizia.

“Katika meelezo nimeona mzee huyu ana mtoto wake wa kike na anafanya kazi katika shirika moja la simu si ndio?”

“Ndio”

“Nahitaji kuanza na huyo mwanaye wa kike”

“Unataka kumteka au kumfanya nini?”

“Ndio ninahitaji kumteka hisia zake, kupitia yeye nitaweza kuingia ndani kabisa katika familia ya mzee Mkumbo”

“Mmmm ni wazo zuri ila je umemuelewesha Camila juu ya jambo hili, isije tukapigana vita ambayo itaturudia sisi wenyewe?”

“Anaelewa kila kitu na nilisha muelez akia aina ya mbinu ambayo ninakwenda kuitumia kuifanya. Kikubwa ni kuhakikisha tunamuangusha mzee huyu”

“Sawa kama ni hivyo basi kila kitu kina wezekana”

“Nitahitaji kufahamu kwa sasa biti huyo yupo wapi ili tujue ni nini anacho kipanga”

“Sawa”

Jojo akafungua laptop tuliyo kuja nayo na kuanza kumtafuta binti huyo kupitia mtandao.

“Sasa hivi namuona hapa anaelekea katika jengo la kibiashara Mlimani City”

“Ndio wapi?”

“Utafadhamu kama ukiamua twende”

“Sawa, linalo wezekana hivi sasa lisingoje baadae”

“Poa, je nibadilishe mavazi haya au?”

Nikamtazama Jojo jinsi alivyo vaa gauni lake refu lililo mpendeza.

“Una suti yoyote labda ulio kuja nayo?”

“Ndio”

“Vaa hiyo basi”

Camila akavaa suti nyeusi iliyo mfanya dhairi aonekane ni mlinzi wangu. Nikavaa koti langu la suti nililo livua muda nilipo kuwa tuna ingia ndani humu. Tukapanda kwenye gari letu tulilo kuja nalo aina ya BMW X6, nikakaa siti ya nyuma huku Jojo akiwa amekaa siti ya mbele kama dereva na nywele zake ndevu akiwa amezibana kwa nyuma huku baadhi ya nywele akiwa ameziachia eneo la usoni mwake na kufunika jicho lake la upande wa kulia. Nikaitazama hii saa ya dhahabu aliyo nikabidhi Dany asubuhi, kwa haraka haraka mtu akinitazama ni lazima atagundua kwamba mimi ni kijana mwenye pesa zangu tena sio chache ni nyingi sana. Nikaanza kupitia sura ya binti huyu wa Poul Mkumbo, ni binti mzuri kwa kukadiria ana umri kama miaka ishirini na tano au na kuendelea hivi, ila kutokana Mungu amenipa umbo kubwa kiasi sio rahisi kunidhania kwamba mimi ni kijana wa miaka kumi na nane.

Tukafika katika jengo la kibiashara la Mlimani City. Jojo akashuka kwenye gari na kunifungulia mlango wa siti ya nyuma ya gar hili,i kisha tukaanza kutembea kuelekea ndani ya jengo hili, kabla ya kufika katika mlango mkubwa wa kuingia ndani ya jengo hili, tukamuona binti wa Poul Mkumbo akitoka huku akiwa ameongozana na walinzi wanne huku wawili wakiwa ni wa kiume huku wengine wawili ni wakike. Wakihakikisha wana mpa ulinzi mkubwa msichana huyu asiweze kusogelewa na mtu wa aina yoyote ile.



Sikuhitaji kumkwepa dada huyu zaidi ya kutembea usawa ambao anatembea yeye, kitendo cha kumkaribia walinzi wake wakajaribu kunizuia, ila Jojo kwa haraka naye akasimama mbele yangu akionyesha msisitizo kwamba nisiguswe na walinzi hawa.

“Samahani”

Nilianza kuzugumza huku nikimtazama msichana huyu.

“Unahitaji nini?”

Binti huyu alizungumza kwa dharau kidogo huku macho yake yakiwa na kazi ya kunishusha na kunipandisha juu na kunishusha chini.

“Ninaweza kuzungumza nawe kwa sekunde kadha?”

“Me……..!!?”

“Ndio”

“Umetokea wapi hadi uhitaji kuzungumza na mimi kwa maana kwanza sikujui na jinsi unavyo endelea kuwa mbele yangu ndivyo jinsi unavyo nipotezea muda. Tuondokeni?”

Dada huyu alizungumza kwa dharau kubwa kisha akaanza kutembea kuelekea walipo acha magari yao. Japo nilipitia maisha ya kunyanyasika kutokana na ubaguzi wa rangi katika nchi ya Ujerumani, ila sijawahi kupitia hali ya kunyanyaswa kama hii tena na mswahili mwenzangu.

“Tuondoke zetu”

Nilimuambia Jojo huku nikiwa nimefedheheka sana moyoni mwangu.

“Hapana tuingie ndani, hivi tutaonekana kama tulikuwa tunamuhitaji yeye”

Nikakubaliana na wazo la Jojo, tukaingia ndani ya jengi hili na kuanza kupita pita kwenye maduka ya nguo. Tukanunua nguo kadhaa, kisha tukarudi hotelini huku mpango wangu wa kwanza ukiwa umegonga mwamba.

“Umekata tamaa ya kuwa na binti huyu?”

“Ana dharua kubwa sana ila dharau yake nina uhakika itakwenda kupotea siku moja”

“Kesho kuna mkutano wa kununua hisa katika kampuni anayo ifanyia kazi. Mwenye kampuni ana hitaji kuiuza kwa matajiri sasa kesho ni muda wa kumuonyesha kwamba wewe unaweza”

Jojo alizungumza huku akiwa ameshikilia simu yake mkononi, akanionyesha juu ya uuzaji wa kampuni hiyo ambayo itagarimu zaidi ya dola za kimarekani bilioni mbili na nusu kwa yule ambaye atahitaji kuinunua nzima, ila kama nitahitaji kuwa mwana hisa basi nitanunua kiasi cha hisa katika kampuni hiyo.

“Nahitaji kununua kampuni nzima?”

“Nzima?”

“Ndio nahitaji kuimiliki na awe chini yangu”

“Hicho kiasi cha pesa unacho?”

“Ndio ninacho, nina makapuni mengi na nina kiasi cha kutosha tu”

“Sawa, kama unahitaji basi tuingize jina lako kwenye watu watakao hudhuria mkutano huo wa kununua hisa za kampuni hiyo”

“Wewe ingiza, kikao kitakuwa ni saa ngapi?”

“Saa mbili asubihi”

“Sawa fanya hivyo nahitaji kutumia simu yako kuwasiliana na dada yangu, je unaweza kunisaidia katika hilo”

“Hakuna shida”

Nikamtafuta Mery kupitia mtandao wa Imo, kwa bahati nzuri nikampata,, nikampigia simu yake na ikaanza kuita, akaipokea na tukaanza kuonana.

“Ethan ni wewe?”

Dada Mery alizungumza huku akiwa amejawa na furaha kubwa sana usoni mwake.

“Yaa ndio mimi”

“Ohoo Mungu wangu, za Tanzania”

“Salama vipi mama anaendeleaje?”

“Mama anaendelea vizuri na nina habari nzuri”

“Habari gani?”

“Timu yako jana imechukua kombe, je ulitazama?”

“Ohoo hapana, weee wameshinda goli ngapi?”

“Goli nne kwa moja, yaani wote walisema kombe hilo ni kwa ajili yako. Hapa nipo nao hotelini huku tunaendelea kushangilia”

“Hahaaa daa wasalimie sana ila usiwaambie kwamba mimi nipo wapi”

“Najua wala usijali kwa hilo jambo. Ehee vipi unaendeleaje?”

“Safi, kesho kuna kampuni nitahitaji kuinunua huku Tanzania”

“Waoo ni jambo zuri mdogo wangu, mimi nitaendelea kukuunga mkono kwa asilimia mia moja. Niambie nini unahitaji?”

“Nilikuwa ninakuap taarifa hata nitakapo toa kiasi cha pesa benki usije ukashangaa”

“Usijali mdogo wangu. Ikiwa baba aliamua kukuachia majukumu yote mikononi mwako. Nafurahi kuona jinsi uanvyo zidi kujitanua kiuchumi”

“Nashukuru dada yangu, basi tutawasiliana kesho pale nitakapo kuwa nimemaliza kufanya biashara hiyo.

“Sawa mdogo wangu kesho”

“Sawa”

Nikakata simu na kumrudishia Jojo simu yake.

“Nimesha ingiza jina lako na langu, mimi nitasimama kama mlinzi wako”

“Sawa dada nashukuru kwa kuniunga mkono”

“Usijali jukumu langu ni kuhakikishakwamba kile tunacho kwenda kukifanya kinafanikiwa kwa asilimia mia moja”

“Sawa”

Usiku wa siku hii Jojo akanitembeza kwenye baadhi ya maeneno ya kumbi za starehe kisha tukarudi hotelini na kulala. Asubihi na mapema tukaanza kujianda huku mimi nikivalia suti ya rangi ya kaki pamoja na shati la blue. Kiufupi nimependeza sana. Jojo akanitengeneza nywele zangu vizuri kisha tukaanza safari ya kuelekea katika kampuni ya ZAirtel. Majira ya saa mbili kasoro tukawasili katika kampuni hii yenye jengo moja refu lenye gorofa zipatano kumi na tano. Tukapokelewa na wahudumu wa kampuni hii ambayo wanapokea wageni rasmi walio kuja kununua hisa za kampuni hii.

Tukapelekwa moja kwa moja hadi ukumbi ambao nikakuta baadhi ya wafanya biashara huku wengine wakiwa ni watu kutoka katika mabara tofauti ikiwemo Ulaya na Asia. Nikakaribisha moja ya kiti huku Jojo akikaa kiti cha nyuma yangu kama mlinzi wangu. Wakaendelea kuingia wafanya biashara wengine, ilipo timu saa mbili kamili asubihi kikao kikaanza. Kila kwenye meza kuna maiki ambayo mtu anaweza kuzungumzia pale atakapo hitaji kutangaza dau lake. Nikamuona mtoto wa Poul Mkumbo akiwa amekaa pembeni ya mmiliki wa kampuni hii ambaye nilimsoma jana usiku asili yake ametokea nchini Afrika kusini.

“Karibuni sana, sasa tunaanza kupokea ofa zenu”

Muendeshaji wa ununuzi wa hisa hizi alizungumza huku dada mmoja akianza kutusambazia karatasi kila mmoja yenye maelezo niliyo anaza kuyasoma taratibu.

Nilipo maliza kuhakikisha kusoma maelezo haya yanayo panga kiwango cha hisa na bei yake nikaendelea kusikiliza ni kitu gani kinacho endelea. Wafanya biashara wezangu ambao wote ni watu wazima wakaanza kutangaza viwango vyao huku wote wakiwa wameanza na dola milioni kumi.

Muda wote macho yangu yapo kwa mtoto wa Poul Mkumbo, adui yangu namba moja, kila ninalo lifanya nina hitaji kuhakikisha kwamba ni moja ya mbinu ya kuhakikisha kwamba nina lipiza kisasi.

“Dola milioni mia tisa”

Muarabu mmoja alizungumza na kuwafanya watu wote tumtazame kwani hadi sasa hivi yeye dau lake ndio lipo juu.

“Dola bilioni moja”

Mama mmoja wa kizungu alizungumza na kufanya macho ya watu kuyahamishia kwake.

“Moja pointi moja moja bilio”

Muarabu huyu alizungumza tena na kuwafanya wafanya biashara wengine kumtazama. Majibizano ya wafanya biashara hawa yakaendelea hadi ikafika dola bilioni moja nukta nane.

“Dola bilioni moja nukta nane kwa mara ya kwanza”

Wafanya biashara wote wakaka kimya, nikageuka na kumtazama Jojo usoni mwake. Jojo akanikonyeza akimaanisha sasa ni muda wangu wa kuhakikisha kwamba ninatangaza dau kubwa la kuweza kuinunua kuampuni hii.

“Dola bolioni moja nukta nane kwa mara ya pili?”

“Dola bilioni moja mbili na nusu?”

Kwa mara ya kwanza nikawafanya watu wote kutazama upande wangu. Macho yakawatoka huku kila mmoja akionekana kushangaa sana kwani ni kiasi kikubwa na ndio kiasi kilicho kusudiwa na mmiliki wa kampuni hii katika kuiuza. Binti wa Poul Mkumbo akanitazama usoni mwangu kwa mshangao mkubwa sana kiasi cha kunifanya nitabasamu kwa dharau.

Hadi inafika mara ya tatu hapakuwa na mfanya biashara yoyote ambaye aliweza kufungua kinywa chake juu ya kiasi nilicho kitangaza. Baada ya kukosenaka mtu aliye weza kunipiku kibiashara, mkutano ukaisha huku nami nikielekezwa kuelekea kwenye ofisi kuu ili kufanya malipo na kuandikishana mkataba wa manunuzi.

“Ninaitwa bwana Josam Zuma, naamini wewe ndio bwana Ethan Klopp?”

“Ndio”

“Naamini jina lako si geni sana kwenye masikio yangu. Wewe ni mchezaji mpira?”

Mmiliki wa kampuni hii alizungumza huku tukiwa tumeshikana mikono.

“Ndio hujakosea mkuu”

“Ohoo nashukuru sana kufanya bishara na kijana mdogo sana ambaye anajiamini sana kama wewe”

“Nashukuru sana”

“Ohoo huyu ni mkurugenzi wa hii kampuni, anaitwa Biyanka Poul Mkumbo”

“Nashukuru kwa kuweza kufahamu”

Biyanka akajawa na kigugumizi kikubwa sana cha kuweza hata kuupokea mkono wangu kwani nina imani anakumbuka kila jambo ambalo amenifanyia jana mchana.

“Vipi Biyanka mbona kama una kigugumizi vipu muna fahamiana?”

“Hapana mkuu. Nashukuru sana kwa kukufahamu Ethan Klopp”

Biyanka alizungumza huku akinishika mkono wangu, nikauminya vizuri mkono wake ikiwa ni ishara moja ya kihuni. Tulipo maliza kutambulishana, nikaanza kufanya hatua za kuhamisha kiasi hichi cha pesa kutoka kwenye akauti yangu moja ya kibiasha na kuanza kuhamishia kwenye akauti ya mmiliki wa kampuni hii. Nilipo maliza zoezi hilo tukaandishikisha mikataba na nikawa mmiliki halali wa kampuni hii.

“Utabaki kuwa mkurugezi wa hii kampuni, kuanzia kesho nitahitaji kuweza kupata ripoti zote za hii kampuni. Kuanzia mauzo, hasara na faida zitokanazo na hii kampuni sawa Biyanka”

Nilitoa maelekezo haya yote mara baada ya kumaliza kuandikishiana mikataba.

“Sawa mkuu”

“Utakabidhi Jojo namba yako ya simu na nitahitaji kuzungumza nawe mambo mengi sana ikiwezekana leo usiku kabla ya kesho”

“Sawa sawa mkuu”

Biyanka akanijibu kwa heshima zote, kiburi na dharua zote alizo kuwa akinifanyia jana usiku zote zimemuisha. Tukarudi hotelini na Jojo huku tukiwa na furaha kubwa sana kwani mpango wetu umekwenda kama vile tulivyo panga.

“Hongera”

“Nashukuru Jojo, nakushukuru sana kwa kile ulicho nifanyia”

“Usijali, huyu binti amesha nipatia namba yake”

“Waoo sasa muda wa kwenda kuwaangusha maadui zangu hivi sasa umewadia. Umeona jinsi dharau zake zilivyo muisha”

“Yaa sasa kama unafanya kweli kweli mapenzi hakikisha kwamba unafanya kweli na ukimpata hakikisha ana kupenda kupitiliza na akisha kolea hakikisha kwamba una mpa pigo kubwa sana yeye na baba yake naamini kwamba huo ndio utakuwa anguko lao umenielewa”

“Nimekuelewa nanitafahanya hivyo kuhakikisha kwamba ninawaangusha chini yeye na familia yake.”



Nilizungumza huku nikiwa nimejawa na tabasamu pana sana usoni mwangu. Jojo akampigia Dany na kumpa habari hii.

“Camila anahitaji kuzungumza nawe”

“Sawa sawa”

Nikaipoke simu hii na kuingia bafuni.

“Niambie mke wangu”

“Safi ehee niambie ni nini kinacho endelea?”

“Mipango inakwenda vizuri na hadi ninavyo zungumza hivi sasa nimenunua kampuni moja ya simu inaitwa ZAiartel”

“Wooo kweli mume wangu?”

“Ndio na kupitia hi kampuni sasa nitaanza kumsogelea audui yangu na nikimtia mikononi basi nitahakikisha kwamba anajutia kwa yale yote ambayo amenifanyia kwenye maisha yangu”

“Sawa mume wangu nina kuamini sana nina imani kwamba huto niangusha”

“Usijali mpenzi wangu nitahakikisha kwamba, tunarudi Ujerumani tukiwa na ushindi mkubwa sana, sawa mama”

“Sawa mume wangu”

“Nitakufahamisha kila jambo ambalo litatokea”

“Sawa mume wangu, nakupa muda na uhuru wa kuweza kufanya jambo lolote ili mradi uhakikishe kwamba una fanikisha kile kitu ambacho unakihitaji kukifanya”

“Nashukuru mke wangu”

Tukamaliza kuzungumza na Camila na kukata simu. Jioni ikawadia na Jojo akawasiliana na Biyanka na kumpa maelekezo ya wapi anaweza kutukuta. Tukajianda ana kueleeka katika hoteli nyingine ambayo nayo ina hadhi ya nyota tano. Biyanka akafika katika eneo hili la hoteli akiwa ameongozana na walinzi wake wa kike, nikamkaribisha kwa furaha pasipo kuonyesha kwamab niliweza kuchukizwa na tabia yake ya kunidharau jana jioni.

“Pole kwa kuweza kukusumbua”

“Usijali mkuu ni jukumu langu nami nakuomba msamaha kwa yale yote ambayo nilikufanyia jana. Kichwa changu kidogo hakikuwa sawa ndio maana yakatoka yale yaloyo tokea”

“Nimekusamehe, ehee kampuni sasa ipo mikononi mwangu, niambie biashara inakwenda vipi na changamoto ni zipi kwa wafanyakazi walipo hivi sasa?”

“Biashara kwa sasa imeweza kuyumba kidogo kwa nchi yetu ya Tanzania. Uchaguzi kidogo umeyumbisha uchumi, ila nina imani raisi ajaye anaweza kufanya mambo mazuri sana na kusimamisha tena uchumi wa hii nchi”

“Ni kweli, japo sipo Tanzania kwa miaka mingi kidogo ila naipenda sana nchi yangu”

“Nafurahi sana kuweza kusika hivyo mkuu”

“Ehee ni nini ambacho natakiwa kuongeza na nini natakiwa kupunguza katika kuhakikisha kwamba ninadumisha kampuni yangu?”

“Kwa haraka haraka mkuu unachotakiwa kukifanya ni kujali maslahi ya wafanyakazi, kwani kwa miezi ya hivi karibuni, kampuni iliweza kupunguza wafanyakazi kutokana na kuyumba. Pili ushindani katika soko, wezetu wenye mitandao wanajua jinsi ya kupangilia ofa zao. Kupangilia matangazo yao, ila sisi tulishindwa kutokana na kuyumba kiuchumi”

“Ohoo sawa hili nitalitazamia kwa jicho la umakini. Ehee jambo jengine?”

“Kitu kingine ni kuwa karibu na serikali, hususani mgombea anaye gombani kiti cha uraisi kwa chama tawala.”

“Ambaye ni baba yako…..”

“Ohoo kumbe umesha mfahamu?”

“Ndio nimemfahamu na mimi ni shabiki yake namba moja na kama atahitaji nimuunge mkono, kwangu haito kuwa shida kabisa nitahakikisha kwamba anashinda kwa kishindo”

“Ohoo asante sana mkuu”

“Niite Ethan, mkuu ni Mungu pekee ila sisi wote tusimame kwa majina yetu”

“Sawa sawa”

Biyanka alizungumza kwa furaha kubwa sana huku moyoni mwangu nikijiapiza kwamba furaha hiyo itakuw ani huzuni na mateso makubwa sana kwake pale nitakapo hakikisha kwamba nimemuweka mikononi baba yake aliye nipotezea wazazi wangu.

“Kesho naomba uitishe kikao na wafanyakazi wote, hata wale wa hali ya chini namaanisha wale wafagizi, nahitaji kuzungumza nao kisha baada ya hapo tutajua nini cha kufanya”

“Sawa sawa Ethan”

“Kitu kingine, kumbuka kwamba mimi ni kijana mdogo sana. Hivyo mambo yangu nayapeleka kasi sana. Uvivu na uzembe ni adui mkubwa sana kwangu. Kama atakuwepo mtu mwenye asili hiyo katika kampuni yangu basi nitahakikisha kwamba ninamtoa mara moja kwenye kazi yangu”

“Usijali bosi kila jambo litakwenda kama vile unavyo hitaji”

“Nafasi yako haito kuwa na mabadiliko yoyote”

“Nashukuru sana Ethan, nitahakikisha kwamba nina ifanya kazi hii kwa uwezo wangu wote hadi pale utakapo nichoka”

“Siwezi kukuchoka”

Nilizungumza huku nikimtazama vizuri Biyanka usoni mwake, ni binti mzuri, anaye jipenda na ana vigezo vyote vya kuitwa mwanamke mzuri, taratibu nikamshika kiganja chake cha mkono wa kulia na kuanza kuupapasa na kidole changu gumba.

“Eth…”

“Ohoo samahani”

Nilizungumza huku nikimuachia kiganja chake.

“Hapana ila kidogo nimejawaliwa aibu”

“Hahaa….vipi shemeji anasemaje?”

“Hapana sina mwanaume Ethan”

“Kwa nini?”

“Bado sijamuona mwanaume wa kuwa naye”

“Mmmmm”

“Kweli wanaume wengi ni wadanganyifu na mimi huwa nina linda heshima yangu na usichana wangu”

“Hongera sana”

“Ahaa kawaida”

Tukazungumza mambo mengi sana katika usiku huu, hadi majira ya saa tano nikamruhusu Biyanka na akaondoka na walinzi wake. Hatukuona sababu ya kuendelea kuwemo hapa hotelini, tukaanza safari ya kurudi katika hoteli yetu.

“Vipi umefanikiwa?”

Jojo aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.

“Asilimia sabini na tano hizo ishirini na tano nitazimalizia siku kadhaa zijazo”

“Kazi nzuri, ila angalia usije ukamsahau Camila kwa maana nimekuona umejiachia sana kwake”

“Hahaa usijali siwezi kumsahau mpenzi wangu, Camila nimekua naye toka topo watoto dogo sana”

“Sawa”

***

Alfajiri na mapema tukafika ofisi, nikamkuta Biyanka pamoja na wafanyakazi kadhaa, nikasalimiana nao na Biyanka akaanza kunitembeza kwenye jengo hili zima la kampuni hii niliyo inunua. Hadi inatimu saa mbili asubuhi tukawwa tumemaliza kulitembea jengo hili. Kama nilivyo agiza ndivyo jinsi Biyanka alivyo fanya. Wafanyakazi wote hadi wafagizi wa hii kampuni wakakusanyika katika ukumbi mkubwa wa kampuni hii. Biyanka akaanzisha kikao cha kampuni hii huku akinitambulisha kuwa ndio mmiliki mpya wa kampuni hii. Wasaa wa mimi kuzungumza ukawadia, taratibu nikasimama kwenye kiti nilicho kikalia na kusimama eneo lenye kipaza sauti. Nikawatazama wafanyakazi hawa kwa sekunde kadhaa kisha nikatabasamu kidogo.

“Habari za asubuhi”

Wafanyakazi wote wakaitikia salamau yangu. Kitu nilicho kigundua kwa haraka juu ya wafanyakazi hawa ni hali ya woga pamoja na kukatishwa tamaa na kazi ambayo wanaifanya.

“Nashukuru kwa uwepo wenu hapa. Machache ambayo nitahitaji kuyazungumza ni mshikamano, umoja, upendo na kufanya kazi kwa juhudi ndio kitu muhimu katika kuhakikisha kwamba maisha yanu yanakuwa mazuri”

“Nitahakikisha kwamba ninapitia mikataba ya kila mfanyakazi mmoja mmoja na wale ambao hawajapewa mikataba nao tutawapa mikataba yao na nitaongeza mshahara ndani ya mwezi ujao.”

Wafanyakazi wote wakapiga makofi huku wakiwa na furaha kubwa sana.

“Napenda kuhakikisha kwamba ndani ya miezi michache kampuni yetu inakuwa ni namba moja kwa mauzo hapa nchini Tanzania, ila mukinipa ushirikiano wenu nina imani kwamba tutafikia malengo hayo ambayo nimewaeleza hivi sasa. Nashukuru sana kwa muda wenu na ninaomba tuendelee na majukumu yetu”

Nilipo maliza kuzungumza wafanyakazi wakaanza kuondoka huku wakiwa na furaha kubwa sana, tukaongozana na Biyanka hadi ofisini kwangu.

“Nani ni mkurugenzi wa waajiriwa?”

“Yupo”

“Basi muambie ahakikishe kwamba mikataba ya wafanyakazi wote inapitiwa upya nikiwa ninaidhibitisha au fanya hivi nahitaji mikataba ya wafanyakazi wote ofisini kwangu”

“Sawa Ethan, ila kuna jambo moja ambalo umelizungumza pale na sasa tupo mwanzoni mwa mwenzi je hadi mwenzu ujao kweli litakuwa limekamilika?”

“Jambo gani?”

“Juu ya kuwaongezea mishahara wafanyakazi?”

“Usijali nitajua ni jinsi gani nitavyo hakikisha kwamba hili swala linakwenda kwenye mstari na hivi benki muna kiasi gai kama kapuni hivi sasa?”

“Pesa ziliszo acha na mmiliki aliye pita ni milioni mia mbili za Kitanzania”

“Hayo ni mauzo ya muda gani?”

“Sio mauzo ya muda, ni pesa alioyo iacha kwenye kampuni ili mmuliki mwengine atakapo kuja aweze kuziendelezea katika kuendesha kampuni”

“Sawa nimekuelewa fanya nilicho kuambia”

“Sawa Ethan”

Biyanka akatoka chumbani humu na kuniacha ofisini kwangu, baada ya dakika kumi, mkurugenzi anaye shuhulika na maswala ya waajiriwa akafika ofisini kwangu akiwa na mikataba ya wafanyakazi wote. Nikamsalimia mwana mama huyu kisha akaanza kunionyesha mikataba ya wafanyakazi wa ngazi za juu ikiwemo wakurugeni wa vitengo vyote.

“Nashukuru mama yangu, niwekee hapo nitaipitia leo”

“Sawa mkuu”

“Niite tu Ethan mama yangu”

“Sawa mimi ninaitwa Bi Agatha Kimaro”

“Ahaa nashukuru mama Kimaro”

“Naweza kuzungumza nawe kidogo?”

“Ndio kuwa huru tu mama yangu”

“Hakika nimependa kile ulicho kizungumza, ni ndani ya dakika mbili ila umezungumza vitu vyenye poiti kubwa na nisikufiche, umenipa moyo wa kuitumikia hii kampuni. Naomba maneno yako yasimame mwanangu katika kile kitu ulicho kusuida kufanya juu yetu na Mungu akubariki mwanangu”

“Nashukuru sana mama, naamini mutazidi kunisaidia”

“Wala usijali katika hilo mama yangu, nipo pamoja nanyi”

Mama Kimaro akatoka ofisini kwangu. Nikaendelea kupitia taarifa kadhaa za kampuni hii, hadi inafika muda wa wafanyakazi kutoka ofisini hapa sikuweza kumaliza kazi nilizo kusudia kumaliza hapa na kunilazimu kuongeza muda wa ziada katika kuifanya kazi. Nikamruhusu Jojo kurudi hotelini na kumpa maagizo ya kuja kunichukua saa tatu usiku. Mida ya saa moja usiku mlango wa ofisi kwangu ukagongwa, nikamruhusu anaye gonga mlango aweze kuingia ndani.

“Ethan kumbe bado hujaondoka?”

Biyanka alizungumza huku akiingia ofisini kwangu. Nikamsindikiza kwa macho hadi kwenye kiti alicho kikalia. Taratibu nikasimama na kuzunguka kwenye meza hii kubwa ya hapa ofisini kwangu, nikakaa juu ya meza huku nikimtazama Biyanka kwa macho makali, taratibu nikamshika kidevu chake kwa kiganja cha mkono wangu wa kulia kisha nikamnyanyua uso wake na tukatazama. Biyanka akasimama taratibu akasimama na mikono yake akaiweka juu ya mapaja yangu huku tukitazamana na midomo yake akianza kuing’ata ng’ata akiashiria kwamba ana haja ya kuhitaji kile nilicho kikusudia kumfanyia na sasa ndege niliye mtega anaanza kuingia kwenye tundu bovu.


Nikaushusha mkono wangu mmoja hadi kiunoni mwake na kumsogeza karibu yangu na tukaendelea kutazamana kwa sekunde kadhaa. Biyanka akayafumba macho yake ikiwa ni ishara ya kuhitaji kupokea lipsi zangu. Taratibu nikazisogeza lipsi zangu hadi kwenye midomo yake, tukazikutanisha ndimi zetu kwa mara ya kwanza na kumfanya Biyanka kusisimka mwili mzima. Japo moyo wangu na hisia zangu zote zipo juu ya Camila ila hapa nipo kazini. Hisia za Biyanka zikazidi kupamba moto na akaanza kufungua vifungo vya shati langu, kabla hajafika kifungo cha tatu kutoka juu nikamshika mkono wake.

“Sehemu hii sio salama, si unajua kuna baadhi ya wafanyakazi wapo bado ofisini”

“Ndio Ethan”

“Tutafute sehemu nyingine ambayo tunaweza kufanya hili jambo”

“Tunaweza kwenda kwangu?”

“Mmmm unaishi na nani?”

“Na dada wa kazi, ila hana shida sana”

“Mmmm ngoja nizungumze na mlinzi wangu akiniruhusu basi nitaweza kuondoka nawe akikataa basi tutafanya siku nyingine”

“Mmm….jamani Ethan nina hamu sana na wewe mpenzi wangu. Usinifanyie hivyo jamani?”

“Ngoja niwasiliane naye mara moja”

Nikamuachia Biyanka na kuzunguka hadi kwenye kiti changu, nikaingiza mkono wangu mmoja kwenye mfuko wa koti la suti yangu ambalo nimeliweka kwenye suti yangu na kutoa simu yangu na kumpigia Jojo.

“Ndio Ethan”

“Upo wapi?”

“Nipo hoteli kuna mambo nayashuhulikia, vipi nije kukuchukua?”

“Hapana, nahitaji kwenda nyumbani kwa Biyanka naamini nitalala huko”

“Mmmmm wewe mtoto, usitake kuniambia kwamba kila jambo ulilo likusudia limekwenda kama vile ulivyo panga”

“Ndio maana yake”

“Duuuu, kuwa makini”

“Nipo makini kuliko unavyo dhania”

“Sawa ujtanijulisha kila jambo na utakapo patwa na tatizo nifahamishe”

“Sawa”

Nikakata simu na kumtazama Biyanka usoni mwake.

“Tunaweza kwenda sasa”

“Kweli?”

“Ndio”

Biyanka kwa haraka akazunguka kwenye hii meza kubwa kiasi, akanikumbatia kwa furaha sana huku machozi yakimlenga lenga usoni mwake.

“Unataka nikupikie nini?”

“Chohote”

“Sawa baba”

Biyanka akaninyonya midomo yangu kwa sekunde kadhaa kisha akabeba koti langu, akanisaidia kupanga vitu juu ya meza yangu kisha tukaondoka katika eneo hili. Tukaelekea katika eneo la maegesho ya magari na kuwakuta walinzi wake wakitusubiria. Tukaondoka eneo hili na kuianza safari ya kuelekea nyumbani kwake.

“Ethan yaani sijui niseme nini?”

“Kivipi?”

“Yaani nashindwa hata kuzielezea hisia zangu juu yako. Unajua toka siku ile tulipo kutana pale Mlimani City nilihisi jambo fulani katika moyo wangu. Ila sikuhitaji kujiaminisha kwa haraka na nikajua ni mambo ya kupita. Sasa siku nilipo kuona kwenye kikao cha kununua hisa, hapo ndipo nilipo ishiwa nguvu kabisa. Yaani haijawahi kutokea kwa mwanaume yoyote ile kuwa naye na hisia kama jinsi nilivyo patwa na hisia kwako”

“Hahaaa usijali nilikupenda nilipo kuona kwenye picha”

“Kwenye picha?”

“Ndio, kumbuka kwamba baba yako ni maarufu sana na nyinyi familia yenu ni maarufu, ila nilipata mashaka kwamba nitakupataje, ikiwa unalindwa namna hii”

“Hahaa jamania, ila unajua ni nini Ethan?”

“Ni nini?”

“Kila jambo kwenye haya maisha linatokea kwa makusudi ya Mungu. Sikutarajia kw kipindi kama hichi kama ninaweza kujiingiza kwenye mahusiano ya kimapenzi na mwanaume yoyote”

Biyanka alizungumza kwa furaha sana, tukaendelea na safari yetu hadi tukadika kwenye nyumba yake nzuri iliyo tengenezwa kwa mtindo mmoja mzuri sana wa gorofa pacha zinazo fanana katika muonekano wa nje.

Tukaingia ndani na kukaribisha na msichana mmoja mzuri.

“Fatuma, huyu ni Ethan. Ethan huyu ni Fatuma, ukiachilia kama mfanyakazi wangu, ila ni mdogo wangu kwa maana nimeishi naye kwa miaka mingi sasa”

“Ohoo nashukuru kukufahamu Fatuma”

“Hata mimi nashukuru kukufahamu Ethan”

“Fatu huyu ni shemeji yako”

Nikamuona Fatuma akistuka kidogo, kisha akatabasamu.

“Ndio ni shemeji yako acha kushangaa”

“Jamani dada kwani nimeshangaa”

“Nakuona macho yamekutoka. Umepika nini?”

“Kama kawaida?”

“Mpenzi amepika kuku na chipsi vipi utakula au niingie jikoni mwenyewe?”

“Hapana, usisumbuke hicho hicho chakula kina tosha”

Fatuma akatukaribisha mezani, Biyanka akapata jukumu la kunihudumia chakula hichi na taratibu tukaanza kula huku tukiwa tumejawa na furaha. Kwa haraka haraka mtu akitutazama anaweza kuhisi tumejuana siku nyingi sana, ila ukweli ni kwamba tumejuana leo na katika mahusiano yetu hatujamaliza hata masaa matano. Matukio yote ya kulishana mimi na Biyanka kwa fatuma yakawa ni mshangao mkubwa sana.

“Shem”

“Bee”

“Mbona una tushangaa sana vipi?”

“Unajua sijawahi kumuona dada yangu akiwa katika hali ya furaha kama leo, ndio maana nina shangaa shemeji yangu”

“Ohoo hajawahi kuleta mchepuko humu ndani?”

“Hata siku moja. Huu unakwenda mwaka wa sita sijawahi kumuona akiwa na mwanaume aliye nitambulisha kwamba ni mpenzi wake”

“Basi mimi ni mwenye bahati”

“Kweli shemeji una bahati kubwa sana”

“Mpenzi wangu twende ndani bwana”

Biyanka alizungumza huku akinishika mkono. Tukanyanyuka kwenye kiti hichi nilicho kalia na tukaanza kuongozana kupandisha gorofani. Tukaingia kwenye moja ya chumba kizuri na kilicho pangiliwa vizuri. Biyanka hakuhitaji hata kunipa sekunde za kujifikiria hichi ninacho kwenda kukifanya, ambacho kwa namna moja ama nyingine ni usaliti kwa Camila.

Akaanza kuninyonya lipsi zangu huku akinivua nguo zangu, nilipo salia na boksa mwilini mwangu, akanisukumia kitandani, kisha naye akaanza kuvua nguo zake. Akapanda kitandani akiwa na bikini tu, kwa jinsi alivyo nona, nikajukuta nikimeza fumba zito la mate.

Akanikalia kiunoni mwangu na tukaanza kunyonyana midomo yetu kiasi cha kunifanya nisisimke sana mwili wagu.

“Ethan”

“Mmmmm”

“Nakupa usichana wangu, nakuomba usije ukanichezea”

“Unataka kuniambia kwamba wewe ni bikra?”

“Ndio”

Nikashusha pumzi taratibu kwani hichi ninacho kwenda kukifanya ni ukatili mkubwa sana kwake, kwani kusema kweli Biyanka ni daraja la mimi kuweza kufanikisha kile kitu ambacho nimekikusudia kukifanya juu ya baba yake.

“Mbona huna raha?”

Swali la Biyanka, likanitoa kwenye msongamano wa mawazo ulio anza kukishika kichwa changu.

“Hapana nipo sawa”

“Una uhakika Ethan”

“Yaa nina uhakika, unajua sikuwahi kufikiria siku hata moja kama nitakuja kupata msichana ambaye amejitunza. Nakuahidi Biyanka wewe ndio mke wangu, nitafanya kila jambo ili mradi uweze kujawa na furaha kwenye maisha yako”

“Nashukuru sana mpenzi wangu”

Biyanka akanivua boksa yangu, akamshika vizuri jogoo wangu huku akionekana kumtamani sana. Pasipo hiyana akamuingiza mdomoni mwake na kuanza kumnyonya taratibu. Nikaanza khisi raha ambayo siku zote huwa nina ihisi pale Camila anavyo nifanyia mchezo huu. Akili na fahamu zangu, zote nikawa nahisi ni Camila ndio anaye nipa burudani hii.

Nikamlaza chali Biyanka na kumvua bikini yake, taratibu nikaanza kumnyonya kitumbua chake na kumfanya aanze kulia kama mtoto mdogo, nikaendelea kumnyonya hadi nilipo jiridhisha mimi mwenyewe, taratibu nikaanza kumpa kitumbua jogoo wangu. Japo kwa mara ya kwanza ni maumivu kidogo kwa Biyanka ila sikulijali hilo kwani sio mara yangu ya kwanza, kumtoa mwanamke bikra.

“Taratibu”

Biyanka alilalama huku akiendelea kusikilizia jinsi ninavyo kishuhulikia kitumbua chake. Mzunguko wa kwanza niliufanya taratibu tena kwa ustadi wa hali ya juu. Hadi tunafika tamati Biyanka hakuweza kulalamika kwa maumivu ya aina yoyote ile. Biyanka akanikumbatia kwa nguvu sana hukua akilia.

“Siamini Ethan”

“Kwa nini?”

“Sijui mpenzi wangu, yaani siamini kama kweli leo usichana wangu umeweza kuondoka jamani”

“Amini tu mpenzi wangu”

Biyanka akanitazama usoni mwangu kwa sekunde kadhaa.

“Ethan”

“Mmmm”

“Ukiniacha haki ya Mungu nitajiua mpenzi wangu”

“Siwezi kufanya kitu kama hicho niamini. Sitaki kufanya dhambi kubwa kama hiyo”

“Hivi Ethan huna mwanamke kweli?”

Nikaka kimya huku nikifikiria nini cha kuzungumza

“Nilikuwa naye, ila kwa sasa hatuna mahusiano kabisa”

“Ulikuwa naye hapa Tanzania?”

“Hapana ni Ujerumani ninapo ishi”

“Ahaa kwa hiyo kwa Tanzania, mimi ni mwanamke wako wa kwanza?”

“Ndio”

“Ohoo asante Mungu kwa kweli”

Biyanka alizungumza huku akiwa amejawa na furaha kubwa sana. Biyanka akaniaga na kuelekea bafuni, gafla nikamuona Ethan akiwa amesimama pembeni ya kitanda hichi.

“Nakuona una kula bata wajina”

“Aisee imenistua sana”

“Pole sana rafiki yangu, kitu ambacho nimekuja kukusisitizia hakikisha kwamba humsahau Camila, unakumbuka maagano ambayo nilikueleza huko nyuma?”

“Ndio, tambua kwamba nipo kazini hata mimi mwenyewe sipendi kumsaliti mpenzi wangu”

“Sawa, zoezi lako lifanye ndani ya muda mchache na uhakikishe kwamba likiisha unamrudia binti wa watu kwa maana kitu ninacho kifanya hivi asa ni kumpa moyo wa uvumilivu na kuto kuwa na wivu mkubwa sana na wewe”

“Nashukuru kwa hilo. Vipi Mery mumefikia wapi?”

“Tunaendelea vizuri”

“Mwanasheria na mke wake, wamefikia wapi?”

“Mmmmm nitakueleza kesho, sasa hivi acha niondoke eneo hili”

Ethan akaondoka eneo hili na kuniacha peke yangu. Biyanka akarudi huku akwia na furaha sana. Akapanda kitandani na akanikumbatia kwa furaha sana.

***

Asubuhi na mapema tukajiandaa na kuelekea kwenye hoteli ambayo ninaishi. Tukaingia katika chumba ninacho ishi na Jojo huku nikiwa nimeongozana na Biyanka. Tukasalimiana na Jojo ambaye tayari tumemkuta akiwa amesha jiandaa kwa kunipeleka ofisini kwa siku ya leo.

“Tayari nguo nimesha kuandalia”

“Sawa sawa nashukuru”

Nikabeba nguo zangu na kuingia bafuni, nikabadilisha nguo na tukaiza safari ya kuelekea ofisini kwangu, huku tukiwa tumepanda gari moja na Biyanka huku gari mbili za walinzi wake zikitutangulia kwa mbele. Tukafika ofisini na kila mmoja akaendele ana majukumu yake. Kitu cha kwanza nilicho anza kukifanya ni kuhakikisha kwamba kila mkataba wa mfanyakazi katika kampuni yangu nina upitia kwa umakini wa hali ya juu. Nilipo maliza kuipitia mikataba yote, nikafanya kikao na wakurugenzi wa vitengo vyote katika hii kampuni na tukapanga mikakati ya jinsi gani tunaweza kuikuza kampuni yetu ndani ya wiki mbili tu. Mikakati niliyo weza kuwapatia kila mmoja aliweza kuridhinika naye na kuamini kwamba kwa muda huo nilio weza kuwapatia basi tunaweza kufanikiwa kwa asilimia kubwa sana. Nikarudi ofisini kwangu huku kichwa changu kikiwa kimechoka kwa kweli kwani kazi niliyo ifanya kwa siku ya leo ni kubwa kuliko kawaida.

“Pole mpenzi wangu kwa kuchoka”

Biyanka alizungumza huku akizunguka meza yangu na kusimama nyuma ya kiti changu na kuanza kuniminya minya mgongoni mwangu.

“Nashukuru mpenzi wangu”

“Nimezungumza na baba leo na nimemueleza juu ya mahusiano yetu na sifa zako zote, ameniomba leo usiku twende nyumbani kwake tukajumuike chakula cha usiku.”

Habari hii kidogo ikanistua sana, kwani sikutarajia kwa haraka hivi ninaweza kukutana na adui yangu ambaye nimejiapiza moyoni mwangu kwamba ni lazima niweze kumfanyia kitu ambacho hakuwahi kufanyiwa kwenye maisha yake yote.



“Mbona umestuka mpenzi wangu vipi?”

“Ni suprize uliyo nifanyia kwa maana sikutarajiua kuweza kukuata na raisi mtarajiwa wa hii nchi”

Nilizungumza kwa unafki kidogo kwani chuki na mipango ya kumuangusha baba yake ni mikali sana.

“Yaa ni kweli nimekufanyia suprize mpenzi wangu, yote nahitaji ufahamu kwamba nina kupenda na kukuhitaji kwenye maisha yangu.”

“Nashukuru sana”

“Ngoja nielekee ofisini kwangu, kuna kitu ninakwenda kukichukua muda si mrefu”

“Sawa”

Biyanka akatoka ofisini humu, nikampigia simu Jojo na kumuomba aweze kufika ofisini kwangu. Baada ya sakika kadha Jojo akaingia na kukaa katika mojawapo ya kiti.

“Mipango inazidi kwenda vizuri”

“Kivipi?”

“Biyanka anahitaji leo twende kwa baba yake”

“Weee”

“Haki ya Mungu vile tunakwenda kupata chakula cha usiku”

“Mmmm sasa hapo kazi inakwenda vizuri. Ila kwa ushauri wangu wa haraka haraka kwako. Hakikisha kwamba hasira yako unaificha, usimuonyeshe ishara ya aina yoyote mzee huyo. Umenielewa?”

“Nimekuelewa”

“Na kigtu kingine nimepokea simu kutoka kwa baba kuna kazi anahitaji niweze kumsaidia kuifanya”

“Kazi gani?”

“Bado hajaniweka bayana ila akinipatia maelezo nitakujulisha”

“Sawa, basi jiandae jioni tunaeleka nyumbani kwao”

“Mmmm unaonaje ukaenda peke yako”

“Peke yangu?”

“Ndio, kumbuka kule ni ukweni kwako kwa uwongo, hivyo unatakiwa kujiandaa vizuri”

“Mmmmm”

“Yaa”

“Sawa kutokana nipo na walinzi wake basi naamini nitakuwa salama”

“Sawa sawa, nikusubirie nje au unaelekea ukiwa na nguo zako”

“Nitakwenda hivi hivi hakuna haja ya kubadilisha nguo”

“Basi acha nieelekee hotelini”

“Sawa”

Jojo akaniaga na kutoka ofisini kwangu, baada ya muda kidogo Biyanka akaingia huku akiwa ameshika faili moja.

“Tunaweza kwenda sasa mpenzi wangu. Tupitie nyumbani kwangu, tujiendae kisha twende huko”

“Mmmm sawa, kwa mimi hivi si nipo poa?”

“Yaa hapo cha kubadilisha labda ni shati, ila tutapitia katika maduka na kununua shati jengine”

Tukaondoka ofisini hapa, tukapita katika moja ya duka la nguo, tukanunua nguo zangu za kuvaa usiku huu kisha tukaelekea nyumbani kwa Biyanka. Tukajiandaa na kuelekea nyumbani kwako, njia nzima Biyanka ametawaliwa na furaha kubwa sana. Furaha ambayo kusema kweli kwa upande wangu nina jiapia ipo siku moja watakuja kulia kilio kimoja cha kusaga meno.

Tukafika katika moja ya jumba la kifahari, ulinzi mkali umeimarishwa kwenye kila eneo la nyumba hii. Tukapokelewa na mwana mama mmoja aliye valia mavazi ya thamani kubwa.

“Huyu ni mama yangu”

Biyanka alinitambulisha, nikampa heshima zote mwana mama huyu, akanikumbatia huku akiwa amejawa na furaha kubwa sana.

“Mama mchumba wangu anaitwa Ethan. Ethan huyu ndio mama yangu mzaa chema.”

“Nashukuru kukufahamu”

“Hata mimi ninashukuru kukufahamu. Karibuni ndani”

Mwana mama huyu alizungumza kwa furaha kubwa sna. Tukaingia ndani, sebleni tukamkuta mzee Poul Mkumbo, akanyanyuka kwenye sofa na kusalimiana nasi kwa furaha.

“Biyanka njoo”

Mama alizungumza na wakaondoka na Biyanka sebleni hapa na kuniacha na mzee huyu.

“Ndio kijana habari yako”

“Salama kabisa baba”

“Umesema unaitwa nani?”

“Ethan Klopp?”

“Ohoo wewe ndio yule kijana mchezaji mpira?”

“Ndio mimi mzee”

“Safi sana sifa zako nimezisikia sikia uwanjani, nina imani kwamba binti yangu amepata kijana mzuri atakaye mjali”

“Ndio muheshimiwa”

Nilizungumza kwa kujikaza tu, ila kusema kweli moyoni mwangu ninajisikia vibaya sana kukaa eneo moja na mzee huyu.

“Ehee niambie asili yako wewe ni nani, umetoka wapi kwa maana sura na muonekano wako ni wakitanzania kabisa”

“Mimi ni Mtanzania kwa kuzaliwa hapa. Walenzi wangu ambao ni mzee Klopp walinichukau kwenye moja ya kituo cha kulelea watoto yatima, nikiwa mdogo sana. Hivyo nimekulia Ujerumani”

“Ahaa kwa hiyo hawakuweza kukuambia maisha yako ya nyuma kwa undani sana?”

“Hapana kwa maana maisha ambayo walinieleza ni kuhusiana kituo hicho cha watoto ya tima na waliniambia kwamba hicho kituo kwa sasa hakipo”

Ilinibidi kuongopea historia ya maisha yangu ya nyuma ili nizidi kuficha uhalisia wangu kwao.

“Ahaa sawa sawa. Ila pole sana kwa kuto weza kuwafahamu wazazi wako”

“Ninashukuru sana mzee”

“Jamani chakula tayari”

Mama alizungumza huku akitutazama.

“Ohoo mkwe twende tukapate ridhiki kidogo”

Tukanyanyuka hapa sebleni na kuelekea kwenye eneo ilipo meza ya chakula. Tukakuka vyakula vingi vikiwa vimeandaliwa. Mimi na Biyanka tukaka kwenye viti vya karibu kabisa huku tukiwa tunatazamana na mama huku mzee Poul Mkumbo akiwa amekaa upane mwengine wa hii meza. Biyanka akaniandalia chakula changu kisha akaanda chakula cha kwake kisha taratibu tukaanza kula taratibu.

“Ethan maswala ya mpira na biashara una yahimili vipi kwa wakati mmoja”

Mzee Poul Mkumbo alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.

“Kila kitu kina ratiba yake. Kutokana bado sijaanza kucheza mpira kama mchezaji maalumu wa timu fulani, hivyo kwa kipindi hichi ninaweza kujali biashara zangu pamoja na makampuni makubwa ambayo nimeachiwa na baba yangu”

“Ahaaa sawa sawa. Una kampuni ngapi?”

“Hii niliyo inunua ni kampuni ya kumi na nne”

“Waooo zote ni mali yako?”

“Kwasasa zipo chini yangu kwa maana baba amenirithisha”

“Sawa sawa”

Tukamaliza kupata chakula cha usiku, mzee Poul Mkombo akaniomba nikazungumze naye katika ofisi yake iliyomo ndani ya jumba lake hili. Tukaingia katika ofisi yake na akanikaribisha kwa furaha sana.

“Kijana wangu kwanza nafurahi sana kuweza kuwa na binti yangu, nina mambo machache ya kuzungumza nawe nikiwa kama baba”

“Sawa sawa mzee”

“Hivi una mpenda kweli mwanangu au upo naye kwa maslahi binafsi ya kibiashara kwa maana ninakwenda kuwa raisi, sasa usije ukaitumia nafasi hiyo kuwa ngao katika serikali yangu nitakayo kwenda kuitengeneza?”

Nikamtazama kwa sekunde kadhaa mzee Poul Mkumbo kisha nikatabasamu.

“Nimempenda binti yako. Na sina mpango wowote wa kumfanya kama ngao katika biashara zangu kwa maana nimewekeza katika nchi karibia zote za barani Ulaya na nina ingiza kiasi kikubwa ana cha pesa hivyo swala la kununua kampuni hapa Tanzania, si kwamba nina shida ya kiuchumi, hapana ni moja tu ya kuifanya serikali yangu iweze kuongeza mapato yake ya kiuchumi kwa kupitia kodi ambayo nitalipa nikiwa kama mmiliki wa kampuni yangu”

“Ahaa sawa sawa, nafurahi kusikia hivyo kijana, je utanisaidia vipi baba yako mkwe katika kuchukua kiti cha uraisi?”

Nikaka kimya huku moyoni mwnagu nikiwa nimejawa na furaha kubwa sana, kwani ndege mjanja anakwenda kuingai kwenye kumi na nane zangu.

“Siasa kama siasa, sijajua siasa za huku Afrika kutokana sijaishi sana miaka mingi. Ila siana inahitaji pesa na kama ni pesa basi isiwe ni pesa ndogo. Pesa nyingi, wananchi wanatakiwa kupata imani kwa yule ambaye wanakwenda kuma dhamana ya kuwaongoza. Hivyo msaada wangu hapo mkubwa utakuwa ni pesa”

Mzee Poul Mkumbo akatingisha kichwa huku akiwa amejawa na furaha.

“Ndio maana sina mashaka kabisa na wewe katika swala zima la kuwa na binti yangu kwa maana ukiona mtu ana uwezo wa kumiliki kampuni zaidi ya kumi na basi ana akili ya ziada”

“Ni kweli”

“Nitataka kujua mpango wako wa kampeni upo vipi, kisha nijue ni jinsi gani ninaweza kukuunga mkono”

“Sawa sawa, sasa hivi tunakwenda kwenye mchujo wa kichama. Huo nimesha anda watu wangu ambao wataniunga mkono na nina imani kwamba jina lango halito katwa”

“Sawa ni mpango mzuru, jina lako likipita basi nitahakikisha kwaba unaichukua ikulu”

“Nafurahi kusikia hivyo na nina kuahidi nitahakikisha kwamba ninakupa nafasi kubwa ya kuweza kuwekeza katika kila jambo ambalo utalihiaji kulifanya hapa Tanzania”

“Nashukuru baba mkwe”

“Ehee vipi mumesha zungumzia swala zima la ndoa yenu?”

“Hapana, ila ukiwa tayari katika kufunga ndoa na Biyanka basi tutawafahamusha”

“Basi niwaombe muwe wavumilivu kidogo, nikisha chukua ikulu basi nitawaruhusu kufunga ndoa”

“Sawa baba”

Tukamaliza mazungumzo na mzee Poul Mkumbo, kisha tukatoka ofisi humu na kurudi sebleni. Tukazungumza mambo mawili matatu na mama mkwe kisha tukaaga na kurudi nyumbani kwa Biyanka.

“Nimefurahi kuoanana na wazazi”

Nilizungumza huku nikivua koti langu la suti na kumkabidhi Biyanka.

“Kweli?”

“Ndio mpenzi wangu. Nimefurahi sana na kuna mambo mengi sana nimeweza kuzungumza na baba, nina imani kwamba nitamsaidia kwa asilimia mia moja kuhakikisha kwamba anaingia ikulu”

“Kweli?”

“Ndio mpenzi wangu, kwa sasa tumesha kuwa familia moja”

“Asante mepenzi wangu”

Biyanka alizungumza huku akinikumbatia kwa nguvu

***

Siku zikazidi kusonge mbele huku kampuni yangu ya mawasiliano ikikua kwa kasi sana. Ndani ya mwenzi mmoja kampuni yangu ikashika namba mbili kwa mauzo kati ya kampuni kumi zinazo shuhulika na maswala ya mawasiliano ya Tanzania. Kama nilivyo waahidi wafanyakazi wangu, nikaongeza mishahara yao kwa asilimia ishirini na tano kwa kila mmoja, jambo lililo zidi kuniletea sifa kubwa kwa wafanya kazi wangu. Kadri siku zilivyo zidi kwenda ndivyo jinsi Biyanka alivyo zidi kunipenda na kuchanganyikiwa kwa penzi langu, kichwani mwangu sikuweza kumsahua Camila, ambaye kila siku huwa nina zungumza naye kupitia simu.

Mzee Poul Mkumbo akafanikiwa kuchaguliwa jina lake kuwa mgombea uraisi katika chama chake cha siasa.

“Ethan”

Niliisikia sauti ya Ethan mwenzangu ikiniita katika ufahamu wangu wa akili

“Ndio”

“Muda wa kurudi Ujerumani sasa una karibia, na biti wa watu hivi sasa anahitaji kuwa nawe, kila siki ninajitahidi kadri ya uwezo wangu kuhakikisha kwamba anakuwa ni mtu mwenye furaha pasipo kuwa nawe”

Nikashusha pumzi yangu huku nikijishika paji langu la uso kwa mkono wangu wa upande wa kulia.

“Huku mipango yangu sasa ndio inakwenda kukamilika”

“Itachukua mud asana”

“Kwa nini sana?”

“Kumbuka kwamba tayari baba Camila amesha shinda uchaguzi na zimebaki wiki chache kabla hajaapishwa kuwa raisi wa Ujerumani”

“Kwa hiyo unataka turudi Ujerumani pasipo mimi kufanya jambo lolote kwa huyu mzee?”

“Ukiwa Ujerumani unaweza kukamilisha mipango yako”

“Kivipi?”

“Kwanza unatakiwa kukipa nguvu chama pinzani kwa siri sana. Pili hakikisha kwamba una wapa mipango yote ya adui yako ambayo anakwenda kuifanya. Unajua kwamba siasa ni vita, pasipo kuwa na silaha basi adui yako hawezi kuanguka”

“Ehee na huyu binti yake je nitaachana naye vipi?”

“Huyo muage muambie kwamba asimamie kampuni kuna mambo yametokea Ujerumani na unahitaji kwenda kuyashuhulikia kwa haraka sana”

“Unahisi kwamba hilo swala atalielewa?”

“Wewe ni mwanaume hakikiasha kwamba ana kuelea na hiyo ndio itakuwa tiketi ya kumuacha”

“Je kampuni yangu akiamua kuisambaratisha kutukana na kulipa kisasi cha mapenzi je itakuwaje?”

“Nitashuhulika naye mimi hapo”

“Utamfanya nini?”

“NITAMUUA”



Nikaa kimya huku nikijifikiria sana kwani maamuzi ambayo anataka kuyachukua Ethan kwa Biyanka kwa namna moja ama nyingine hastahili kufanyiwa hivyo.

“Unahisi kumuua Biyanka ni muhimu kweli?”

“Nitamuua pale atakapo hitaji kulipiza kisasi juu yako”

“Ahaa hapo sawa, ila kabla sijaondoka nchini Tanzania nitahitaji kufanya jambo moja”

“Jambo gani?”

“Nahitaji kukutana na mgombea uraisi wa chama pinzani, ninahitaji kuzungumza naye mambo mawili matatu”

“Sawa ila hakikisha kwamba unakutana naye kisiri”

“Sawa, ila nitaonana naye vipi ikiwa Jojo simuoni kwa sasa toka alivyo niaga hadi sasa sina mawasiliano naye?”

“Ngoja nitakufahamisha baadaye jinsi ya kuonana naye”

“Sawa”

Ethan akandoka na nikabaki peke yangu ofisini. Mlango ukafunguliwa na akaingia Biyanka huku akionekana akiwa na furaha kubwa sana kwani kitendo cha baba yake kuchaguliwa kuw amgombea uraisi wa chama tawala basi ni moja ya sifa kubwa sana kwenye familia yao.

“Mume wangu unaendeleaje?”

Biyanka alizungumza huku akizunguka kwenye meza yangu, akanibusu mdomoni mwangu kwa furaha sana.

“Salama mama watoto”

“Ahaa nimekuja kukuomba ruhusa mara moja”

“Ruhusa gani?”

“Kuna mkutano wa wamama, kidogo mama anakwenda kuzungumza nao hivyo ameomba nimsindikize, si unajua maswala ya kampeni”

“Ahaa sawa sawa, unaweza kwenda. Mimi nitaelekea hotelini nikitoka hapa. Kama utapata nafasi basi unaweza kufika”

“Usijali mpenzi wangu tutawasiliana”

“Sawa”

Tukanyonyana lipsi zetu na Biyanka kisha akatoka ofisini kwangu, nikachukua simu yangu na kumpigia Camila, simu yake ikaita hadi ikakatika, nikarudia kupiga kwa mara ya pili ikaita kwa sekunde kadhaa kisha akapokea.

“Niambie mpenzi wangu?”

“Safi mume wangu vipi?”

“Poa, unendeleaje?”

“Ninaendelea hivyo hivyo”

“Kwa nini hivyo hivyo?”

“Nina hamu na wewe mume wangu, nimechoka kukaa huku porini peke yangu. Nahitaji kuja huko huko Dar es Salaam au nirudi nyumbani Ujerumani”

Maneno ya Camila yakanifanya nikae kimya kwa sekunde kadhaa huku nikifikiria ni nini cha kuzungumza.

“Mpango ninakwenda kuukamilisha mpenzi wnagu, ninaomba muda kidogo wa kuvumilia. Sawa mama?”

“Sawa, ila lini utakwisha mpango?”

“Ndani ya wiki moja hivi au mbili”

“Nakupa wiki moja ya mwisho. Ninahitaji haki yangu mume wangu, nimekuwa ni mtu wa kufanya mazoezi magumu ili tu nipoteze hamu ya kufanya mapenzi, tafadhali Ethan naomba nije”

“Sawa mpenzi wangu. Hivi Jojo yupo huko?”

“Nilimuona wiki kadhaa zilizo pita, kwani huko hayupo?”

“Hayupo”

“Unaishije peke yako sasa huko?”

“Nimesha yazoea maisha ya hapa mpenzi wangu”

“Hapana, kesho ninamuomba Dany aniletea huko”

“Kesho”

“Ndio kesho, sahau mambo ya wili moja niliyo kueleza. Kwaheri mume wangu, ninamalizia kufanya mazoezi”

Camila akakata simu na kujikuta mwili wangu mzima ukianza kujawa na joto kali, jasho likaanza kunitiririka usoni mwangu hadi nikajikuta nikivua koti langu la suti. Nikanyanyuka na kuanza kuzunguka zunguka ndani ya ofisi yangu, kwani ujio wa Camila jijini Dar es Salaam unaweza kuniharibia mipango yangu yote niliyo ipanga. Nikapata wazo la kumpigia Dany simu yake, nikaitafuta namba yake na kuipata, nikampigia, simu yake ikaita baada ya muda akapokea.

“Ndio Dany”

“Vipi mbona unazungumza kama una wasiwasi mwingi”

“Nina shida”

“Shida gani?”

“Nimetoka kuzungumza na mke wangu hivi sasa, keso anahitaki kuja Dar es Salaam, sasa mpango wangu bado sijaumaliza utanisaidiaje katika hilo ndugu yangu?”

“Ni kweli alisha nieleza hilo jambo leo asubuhi, sasa wewe unatakeje?”

“Nahitaji umlete baada ya wiki moja?”

“Mmmmm sawa nitajaribu, kwa maana hivi sasa mke amekuwa ni king’ang’anizi na anahitaji kuondoka huku”

“Naomba unisaidie kwa kweli”

“Sawa nitajaribu”

“Nashukuru sana”

Nikakata simu, nikatoa kitambaa changu mfukoni na kujifuta jasho langu usoni, hamu ya kukaa ofisini hapa ikaniisha kabisa, nikachukua koti langu na kutoka. Nikiwa katika kordo nikakutana na wadada wawili walio umbika vizuri sana na wamevalia sare za wahudumu wa wateja mapokezi.

“Habari yako mkurugenzi”

“Salama, aahaaa…mune elekea wapi?”

“Ofisi ya meneja masoko”

Nikajifikiria kwa muda kidogo.

“Leo ni lini?”

“Ijumaa”

“Okay nani anaye fahamu sehemu inaitwa Bagamoyo?”

Mabinti hawa wakatazamana huku wakitabasamu.

“Sote tunapafahamu”

“Okay, sasa kesho naomba kama hamto jali tuweze kuelekea pamoja kwa maana nahitaji kutembea tembea eneo hilo na mimi ni mgeni hapa jijini Dar es Salaam”

“Sawa mkurugenzi hakuna tatizo”

Nikatoa waleti yangu mfuko wa nyuma na kutoa kadi ya biashara zenye namba zangu za simu nikawakabidhi kila mmoja kadi yake, wasichana hawa wakaonekana kufurahi sana kwani namba yangu ni adimu kwa wafanyakazi wa kawaida.

“Ila musimueleze mtu yoyote juu ya hili swala sawa”

“Sawa mkurugenzi, siri yako ipo salama kwetu”

“Nashukuru. Muna magari?”

“Hapana”

Nikatoa noti mbili za dola mia moja, nikawakabidhi kila mmoja.

“Kesho saa nne mutanipigia simu na nitawaelekeza wapi kwa kuja sawa”

“Sawa mkurugenzi”

Wasichana hawa wakazidi kufurahi, hakika Tanzania ina wanawake wazuri sana. Nikaachana hao huku kwa mara kadhaa nikigeuka nyuma, nikaingia kwenye lifti, na moja kwa moja ikanipeleka hadi chini ya ardhi ambapo ndipo yalipo maegesho ya magari ya wafanyakazi wa kampuni hii. Nikaanza kutembea kuelekea kwenye gari langu nilipo liacha, nikiwa hatua chache kutoka lilipo gari langu nikahisi kuna mtu ananifwata nyuma. Nikasimama kisha nikageuka, ila sikuweza kumkuta mtu yoyote, wasiwasi kidogo ukaanza kuniingia kwani eneo hili limetulia na halina watu kabisa zaidi ya magari mengi yapatayo zaidi ya mia moja.

Nikaanza kutemebea kwa mwendo wa haraka hadi kwenye gari langu, nikatoa funguo mfukoni mwangu na kufungua mlango wa gari kisha nikaingia ndani huku nikijaribu kutazama eneo nilipo toka ili niweze kumuona mtu ambaye alikuwa ananifwatilia.

Nikawasha gari hili na taratibu nikaanza kuondoka katika eneo hili, kabla sijafika katika mlango wa kutokea, gafla mbele yangu akasimama mtoto mdogo mwenye umri kama miaka minne au mitano hivi, jambo ambalo lilinilazimu kufunga breki za gafla ili nisimgonge.

Mtoto huyu akabaki akiwa ameduwaa tu huku hali yake akionekana kudhohofika kwa shida, kwani mavazi yake ni machafu kiasi. Nikashika kitasa cha kufungulia mlango ila roho yangu ikasita kabisa kufungua mlango kwani sifahamu huyu mtoto ameandamana na nani. Nikampigia honi kadhaa, ila mtoto huyu hakusogeza zaidi ya kumwagikwa na machozi usoni mwake.

‘Ametumwa au?’

Nilizungumza huku nikigeuka na kutazama pande zote za eneo hili ila sikuweza kumuona mtu yoyote. Nikatoa simu yangu mfukoni na kuwapigia walinzi wa eneo hili, nikawaomba waje eneo hili la maegesho ya magari haraka sana, walinzi hawakuchukua muda mrefu sana wakafika nami ndipo nikatoka kwenye gari hili.

“Ninamshangaa huyo mtoto amekataa kutoka mbele ya gari langu kabisa”

Niliwambia walinzi hawa mara baada ya kumtoa mtoto huyu mbele ya gari langu.

“Wewe umeingiaje ingiaje humu?”

Mlinzi mmoja alimuuliza kwa kufoka sana.

“Usimfokee hembu mlete”

Nilizungumza kwa upole, mlinzi huyu akamleta mtoto huyu sehemu nilipo simama. Taratibu nikachuchumaa ili niweze kuwa kimo sawa na huyu mtoto, ambaye katika kumtazama kwa ukaribu nikagundua ni mtoto wa kike.

“Unaitwa nani?”

Mtoto huyu akabaki akinitazama huku akiendelea kulia sana kwa uchungu, jambo lililo tushangaza watu wote katika eneo hili.

“Binti usilie ehee”

Nilizungumza huku nikitoa kitambaa changu na kuanza kumfuta machozi yake usoni.

“Unaitwa nani?”

Binti huyu hukunijibu zaidi ya kunishika shavu langu la upande wa kulia, taratibu akanikumbatia kwa nguvu sana huku akiendelea kulia. Akatoa kipande cha gazeti kwenye mfuko wa suruali yake hii iliyo chakaa, akanikabidhi kipande hichi cha gazeti, tartibu nikakifungua, sikuamini macho yangu mara baada ya kukuta picha yangu nikiwa uwanjani na timu ya shule ninayo soma.

“Mimi ni shabiki yako”

Alizungumza kwa upole sana huku machozi yakimwagika usoni mwangu, nikajikuta nikilengwa lengwa na machozi huku nikimuonea huruma sana huyu binti.

“Nimelitunza hilo gazeti, na jana nilipo kuwa nina omba omba nje ya geti la ofisi yako nilikuona, nilijua nimekufananisha kumbe ni kweli wewe ndio Ethan ohooo”

Binti huyu alizungumza kwa upole na uchungu sana, akanikumbatia tena huku akilia sana. Nikajikuta nami nikimwagikwa na machozi. Sikujali harufu ya uchafu inayo mtoka binti huyu, nikaendelea kukumbatiana naye hivyo hivyo. Nikamnyanyua binti huyu na kuanza kutembea naye hadi kwenye gari langu.

“Unaitwa nani?”

“Clara”

“Ohoo Clara?”

“Ndio”

“Una jina zuri sana, nyumbani ni wapi?”

Binti huyu akaka kimya kwa sekunde kadhaa huku akinitazama usoni mwangu. Akatingisha kichwa jambo lililo nifanya nimshange kidogo.

“Uma…maanisha nini?”

“Mimi ni omba omba, sina nyumbani kokote mimi nina lala. Hayo ndio maisha yangu”

Nikahisi maumivu makali sana moyoni mwangu, kwani binti mdogo kama huyu hana makazi maalumu.

“Wazazi wapo wapi?”

“Walisha fariki miaka miwili iliyo pita, walipata ajali ya gari hivyo baba mdogo alinichukua na kunilea, ila kwa mateso walio kuwa wakinipatia yeye na mke wake niliamua kutoroka nyumbani na walichukua kila kitu cha baba yangu na kuniacha kama hivi nilivyo”

Maneno ya binti huyu yakazidi kuniumiza moyo wangu. Akafunua shati lake mgongoni, mimi na walinzi wote tukabaki tumejawa na mshangao, kwani ana makovu ya majeraha mengi sana, kiasi kilicho nifanya nizidi kumwagikwa na machozi.

“Baba yako mdogo yupo wapi?”

“Anaishi Mbezi kwenye nyumba ya baba”

“Mbezi ni wapi?”

Niliwauliza walinzi hawa huku nikiwatazama kwenye nyuso zao.

“Zipo Mbezi mbili, ni Mbezi Beach au Mbezi ya kimara mtoto?”

Mlinzi alimuuliza mtoto huyu huku akimtazama usoni mwake.

“Mbezi ya chini”

“Ndio ipi?”

Niliwauliza walilinzi.

“Hapo anazungumzia Mbezi ya Kimara”

“Si unapakumbuka nyumbani?”

“Ehee napakumbuka”

“Wewe na wewe ingieni kwenye gari tuelekee huko”

“Sawa mkurugenzi”

Tukaingia kwenye gari na walinzi wa kampuni yangu na taratibu tukaianza safari ya kuelekea Mbezi ya kimara huku Clara akituelekeza njia ya kuweza kufika kwao.



“Mkurugenzi”

Mlinzi niliye kaa naye siti ya mbele aliniita kwa sauti ya upole, nikamuitikia huku nikimtazama usoni mwake.

“Bila ya kukuvunjia heshima, nina wazo”

“Zungumza tu”

“Kwa mtazamao wangu ninaona kuelekea nyumbani kwa huyu binti sio jambo sahihi, unaonaje tukaanza na taratibu za kisheria kwa mfuno kuelekea polisi, kule kuna kitengo kabisa kinashuhulika na watoto wa aina hiyo na tukitoka huko basi tutakuwa na hata nguvu ya kuelekea kwao”

Nikajifikiria kwa muda kwani wazo hili alilo litoa huyu mlinzi wa kampuni yangu ni zuri sana.

“Alfau kweli, sasa tunaelekea katika kituo gani cha polisi?”

“Kituo kikuu cha kati nina imani kwamba ndio kituo kizuri, wanaweza kusikiliza shida yetu”

“Sawa nielekezeni”

Mlinzi huyu akaanza kunielekeza njia za kupita kwa maana jiji hili la Dar es Salaam, mimi bado ni mgeni kwa baadhi ya maeneo. Tukafika katika kituo hicho, tukakaguliwa kabla ya kuingia ndani. Baadhi ya askari walianza kuulizana mara baada ya kuniona nikiwa nimesimama kwenye moja ya foleni huku nikiwa nimemshika mkono Clara.

“Samahani kaka sogea hapa”

Askari mmoja wa kike ambaye yupo eneo la mapokezi aliniita, taratibu tukasogea eneo alipo.

“Tuwasaidie nini?”

“Ahaa kuna swala la huyu binti hapa, kama tunaweza kuzungumza ofisini basi ningeomba msaada huo”

“Afande Mwanaidi hembu mchukue huyu kaka na mukafanye mazungumzo naye ofisini”

Afande huyu wa kike alitoa maelekezo kwa mwenzake, tukaongozana na Afande Mwanaidi hadi kwenye moja ya ofisi, akatukaribisha na tukaketi kwenye viti vilivyomo katika eneo hili. Nikanza kuelezea jinsi nilivyo kutana na mtoto huyu, kisha Mery naye akahojiwa historia ya maisha yake. Kila ambacho ytulikizungumza afande Mwanaidi alikiandika kwenye faili.

“Nisubirini”

Afande Mwanaidi alizungumza huku akinyanyuka kwenye kiti chake na tukatoka ndani ofisi hii. Baada ya muda kidogo akarejea na baba mtu mzima mwenye kitambi kikubwa kiasi huku begani mwake akiwa na nyota kadhaa ambazo sifahamu ana cheo gani katika jeshi hili la polisi.

“Kijana kwa maelezo niliyo pewa ni kwamba umemuokota huyu binti”

“Ndio hujakosea mzee”

“Sawa. Binti unapakumbuka kwenu?”

“Ndio”

“Mwanaidi andaa askari wanne ninakuja”

“Sawa mkuu”

Afande Mwanaidi akatoka humu na kutuacha na huyu mzee.

“Naitwa Kimaro ni mkuu wa polisi kanda maalumu”

“Nashukuru kukufahamu mzee mimi ninaitwa Ethan”

“Sura yako sio ngeni machoni mwangu. Wewe ndio yule mchezaji wa mpira?”

“Ndio mimi”

“Ohoo karibu sana Tanzania”

“Nashukuru, kuna jambo jengine ambalo hatukukueleza afande aliye toka. Kuna haya makovu mgongoni mwa huyu binti hakika yameniumia sana moyo wangu”

Nilizungumza huku nikiinyanyua tisheti hii ya Clara mgongoni mwake, mkuu wa polisi akashikwa na butwaa, kwani ni makovu makubwa sana.

“Yaani kwa uzee wangu wote huu na mambo mengi niliyo pitia katika jeshi la polisi ila sijawahi kuwa na makovu kama haya. Aisee kuna watu wanyama sana hapa duniani. Binti aliye fanya hivi ni nani?”

“Baba mdogo na mke wake”

Mlango ukafunguliwa akaingia afande Mwanaidi.

“Mkuu tayari”

“Sawa ninakuja”

 ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

BLOG