Search This Blog

Wednesday, November 18, 2020

SIN SEASON 1 SEHEMU YA 4/10

  


SIN SEASON 1

WRITER…………………………………………EDDAZARIA G.MSULWA
WEBSITE………………………………………… www.storyzaeddytz.com
CONTACT……………………………………….. 0657072588/0768516188
AGE……………..18+

SEHEMU YA 4 KATI YA 10


Alfajiri na mapema Magreth akajianda kwa ajili ya kuelekea kazini kwake. Hakumruhusu Evans kufanya kazi kwani bado mwili wake uma majera na maumivu.

“Kua makini mke wangu”

Evans alizungumza huku akijfunika shuka lake vizuri”

“Nashukuru mume wangu. Kila kitu kipo kwenye friji kama uta kupika basi nina imani una weza”

“Ndio mke wangu”

Magreth akafungua mfuko wenye pesa na kutoa kiasi cha laki mbili na kumkabidhi Evans.

“Kilinda wallet mume wangu, usije ukataka kutoka kwenda sehemu uka shindwa kwenda. Simu yako ipo kwenye droo ya hapo pembeni ya kitanda”

“Nashukuru sana mke wangu. Siku nyingine usiwe una hatarisha usalama wako kwa kutembea kwa pesa nyingi kiasi hicho si una fahamu kwamba hali ya kiusalama kwa sasa ni ndogo”

“Ni kweli mume wangu, ila si siku ya kwanza. Ila hapa nikitoka hapa breki ya kwanza ni benki kisha ndio niende kazini”

“Sawa mke wangu”

“Nakupenda sana Evans wangu”

“Nina kupenda pia mke wangu”

Magreth akambusu Evans mdomoni mwake kisha akavaa mkanda wapochi yake.

“Mume naomba msaada wa kunifungulia geti”

“Wala usijali katika hilo”

Wakatoka nje na Magreth akaingia kwenye gari lake. Akauweka mfuko huo wa pesa katika siti ya pembeni, Evans mara baada ya kufungu geti akaondoka na kumuacha Evans akifunga geti la nyumba hiyo. Magreth akawahi kufika benki na kukuta ndio kwanza ina funguliwa. Baada ya mlinzi kuruhusu wateja kuingia, Magreth akawa wa kwanza kuingia ndani ya benki hiyo. Akachukua kikaratasi cha kuhifadhia pesa, akaandika kiasi cha pesa alicho nacho na kuelekea katika dirisha la mhudumu.

“Mage”

Dada huyo alimfurahia kana kwamba ana mfahamu.

“Habari yako”

“Salama tu, naamini una shangaa nime kujuaje. Mimi ni miongoni mwa wateja wako wa chakula pale mgahawani”

“Ahaaa….waoo nashukuru kukufahamu”

“Hata mimi nashukuru kwa chakula kitamu sana unacho kipika yaani. Jana nilipo kila mchana, nikasema hapana, lazima usiku niurudi kukila tena. Haki ya Mungu, wewe dada una mkono wa kupika.”

Muhudumu huyo alizungumza kwa furaha huku akichukua vibunda vya pesa za Magreth, akaziingiza kwenye mashine ya kuhesabia pesa na ikaanza kufanya kazi ya kuhesabu.

“Nashukuru na karibu sana”

“Usijali leo nita washawishi karibi ofisi nzima. Lunch uta tuona pale”

“Asante sana, ukiniletea zaidi ya watu kumi muta lipa asilimia hamsini tu ya bili ambayo muta tumia”

“Kweli Mage?”

“Haki ya Mungu, wewe fanya hivyo”

“Basi usijali, nitakuja na rafiki zangu mida ya saa saba saba hivi mchana.”

“Karibuni sana, una itwa nani?”

“Aziza, nahisi kwamba huwezi kulishau jina langu”

“Siwezi kwa kweli”

Azazia akamaliza kusaini na kupiga muhuri katika karatasi hiyo ya kuhifadhia pesa ikiwa ni ishara kwamba ame zipokea pesa hizo.

“Leo niwapikie nini?”

“Yaani wewe fanya kama jana, yaani hapana. Nimekula kwenye mahoteli makubwa na migaha mingi hapa jijini Dar es Salaam ila sijawahi kukutana na chakula kitamu kama chakula chako”

“Nashukuru sana Azazi. Acha uendelee na majukumu naona wateja wamesha anza kupanga foleni”

“Sawa Mage karibu sana”

“Nashukuru sana”

Magreth mara baada ya kupokea risiti hiyo akatoka ndani ya beki hiyo. Akaingia ndani ya gari lake, kabla hata hajaliwasha simu yake ikaanza kuita, akaitazama vizuri na kukuta ninamba ya Vivian.

“Habari za asubuhi dada Vivian?”

Magreth alizungumza kwa furaha mara baada ya kuipokea simu hiyo”

“Safi ume amkaje?”

“Nimeamka salama dada yangu. Sijui kwa upende wako?”

“Mimi nime amka salama salmini. Sasa una weza kufika hapa Morocco?”

“Ndio nina weza kufika”

“Basi njoo, ukifika hapo nita kuelekeza ni gorofa gani ambalo uje”

“Sawa, ila niambie ni gorofa gani hapo nifike”

“Ukifika hapo mataa uta ona kuna goroa refu kuliko yote na vioo vyake vina rangi ya blue bahari. Hapo ndipo makao makuu ya ofisi za kampuni ya baba yangu”

“Sawa nina fika hapo”

Magreth akawasha gari lake, ila kabla hajaondoka akamuona bi Ngedere akija eneo alipo simamisha gari lake huku akionekana akiwa katika mishe mishe zake.Magreth akapiga honi huku akifungua kioo cha gari hilo.

“Weweeee!!!”

Bi Ngedere alizungumza kwa mshangao huku akimtazama Magreth usoni mwake.

“Ndio ni mimi, shikamoo”

“Marahaba mwanangu hujambo?”

Bi Ngedere aliifurahia salamu hiyo tofauti na siku zote alizo wahi kupewa salamau hiyo na Magreth.

“Sijambo, haya wapi asubuhi asubuhi hii?”

“Naenda hapo benki kukopa”

“Unakwenda kukopa kiasi gani mama yangu?”

“Laki tatu tu kuna vijora nataka nikanunue kwa ajili ya harusi ya yule mtoto wa mdogo wangu . Hivyo niliahidi kujitolea vijora hivyo vivyo inabidi nitoe na isitoshe sherehe ni wiki ijayo”

“Hahaaa…..bi Ngedere bwana hembu ingia kwanza kwenye gari”

Bi Ngedere kwa haraka haraka akazunguka upande wa pili wa gari hilo huku akilishangaa sana.

“Huu mlango wafungukaje, kwa maana ushamba huu”

Maneno ya bi Ngedere yakamfanya Magreth kufurahi kidogo huku akimsaidia kuufunga mlango wa gari hilo kwa ndani na bi Ngedere akaingia.

“Hee Mage hivi hili gari ni lako au?”

“Ndio ni langu mbona una shangaa shangaa?”

“Mmmm umejitahidi mwanagu. Hivi ni danga gani hilo umelipata hadi maisha yamebedilika kwa kiasi hichi kwa maana sisi kule mtaani ndio tunazidi kufulia”

“Hahaa hakuna cha danga wala nini, ni kumuomba Mungu. Kuwa na heshima kwa wako na kukaza buti basi. Tatizo lako umejawa na maneno mengi na vitendo ni sifuri”

“Mmmm alafuni ni kweli shosti yangu ila ndio hivyo si unajua uswahili na maisha bila unafki hayahendi”

“Hahaa haya. Basi hiyo laki tatu mimi nita kupatia. Ila kwa sasa nikupeleke kwenye mgahawa wangu, nikuache hapo kisha nikirudi kwenye mizunguko yangu, basi nita kupatia. Ila siku nyingine bi Ngedere usikope alafu pesa ukafanyia sherehe. Ita kugarimu na kujikuta una uza nyumba kwa laki tanu”

“Nashukuru sana mwanangu. Mungu akubariki”

“Amen”

Magreth alizungumza huku akiwasha gari lake na kuondoka eneo hilo kwa mwendo wa tartaibu taratibu.

“Mashosti zangu wana endeleaje?”

“Mmmm wapo tu, hawana pa kwenda na waume zao walio fulia”

“Hahaaa haya bwana”

Magreth na bi Ngedere wakafika kwenye mgahawa wake. Magreth akasalimiana na wafanyakazi wake. Akamkabidhi bi Ngedere kwa wafanyakazi hao na kuwaomba wamuhudumie kitu chochote ambacho bi Ngedere ata hitaji. Magreth akaeleka katika ofisi zilizopo katika eneo la Morocco. Akaelekea hadi katika ofisi za kampuni ya MORRIS GROP’S OF CAMPANY na akakaribishwa kwa furaha sana na Vivian.

“Karibu sana Mage. Baba yupo ofisini kwake ana kusubiria”

“Nashukuru sana”

Vivian na Mage wakaingia katika ofisi ya mzee Morris. Wakasalimiana kwa furaha kisha mazungumzo yakaanza.

“Mage tuna fahamu kwamba hii biashara yako ni mpya. Ila ume toka kupata wateja wengi sana na kwa muda mfupi sana. Nimatarajio yangu kwamba tukikupa dili la kufanya kakampuni yetu basi wateja wana weza kuongezeka na kuwa wengi kama ilivyo kuwa kwako?”

“Ni kweli”

“Basi tuna hitaji kufanya kazi ya wewe kututangazia kampuni yetu na bishaa zetu tuna imani kwamba tuta kutangaza wewe na sisi tuta tangazika zaidi”

“Sawa sawa. Je mume panga kukulipa kiasi gani?”

“Ahaa Mage tulishauriana na baba kwamba tuanze kukulipa kiasi cha milioni mia moja. Je wewe una afikiana na kiasi hicho kwa maana nia uhakika wa asilimia mia moja kwamba milioni mia moja zetu hatuendi kuzitupa katika hili”

Magreth akashusha pumzi taratibu huku akimtazama mzee Morris na Vivian ambao wana subiria jibu la Magreth kwa hamu kubwa sana.


***

Tomas, mke wake na mwanaye wakaingia kwenye taksi na kuianza safari ya kueleka katika nyumba anayo ishimke wake. Wakafika nyumbani hapo na Tomas akamkabidhi mke wake mtoto wao ambaye tayari amesha zinduka kutoka usingizini. Tomas akaanza kugongwa kwa nguvu mlango huo. Kijana huyo mwenye asili ya kizungu akafungua mlango huo huku akionekana kujawa na mawenge ya usingizi.

“Umerudi tena wewe malaya?”

Mac alizungumza huku akimtazama mke wa Tomas. Tomas hakusubiria hata mke wake ajibu shambulizo hilo la maneno. Akamsukumia ndani Mac na akapepesuka na kuanguka chini. Tomas kwa haraka akamrukia na kumkalia tumboni mwake na kuanza kumshushia makonde ya haja. Mazoezi aliyo pewa na Scooby doo, hakika yalimuwezesha kumdhidi mbinu Mac ambaye ana jaribu kufurukuta eneo hilo la chini alipo anguka.

“Tomasa uta ua, utaua mume wangu”

Mke wa Tomas alizungumza huku akimziba mwanaye sura ili asiweze kushuhudia kipigo hicho anacho patiwa baba yake wa kambo ambaye siku zote ame zoea kumuona hapo.

“Acha nimfunze adabu huyu”

Tomas alizungumza huku akizidi kushushia ngumi za uso kijana huyo wa kizungu.

“Nisamehee kaka”

Mac aliomba msamaha mara baada ya kuona hali ime kuwa ngumu kwake. Msamaha hau oka mfanya Tomas kusitisha mashambulizi hayo na akanyanyuka huku akitazama uso wa Mac jinsi unavyo churuzikwa na damu.

“Ndani ya dakika tano nahitaji utoke ndani kwangu sasa wewe kenge?”

Tomas alizungumza kwa kufoka hukua kimtazama Mac anaye jizoa zoa chini hapo.

“Ha…ahhaaa…ahya”

Mac alizugumza hukua akijikaza kunyanyuka chini hapo. Mac akaanza kutembea kwa kuyumba huku akielekea chumbani, ila kabla hajafika chumbani akaingia jikoni na kuchukua kisu kirefu na siku zote huwa hawapendi watu weusi na ana anaamini kwamba watu weusi ni mbwa ambao hawawezi kuwa juu ya wazungu.

“Tomas nyuma yako”

Mke wa Tomas alitoa ukelele mara baada ya kumuona Mac akija kwa kasi na kutaka kumchoma kisu cha mgongoni. Tomas kwa haraka akageuka na uuwahi mkono wa Mac ulio shika kisu hicho, akaugeuza kwa kasi sana na Mac akajikuta juhudi zate za kuhititaji kumdhuru Tomas kwa kisu hicho, kikitua tumboni mwkae na macho yakamtoka. Tomas akazidi kukishindilia kisu hicho tumboni mwa Mac na kusababisha damu nyingi kuanza kumwagika chini.



Mke wa Tomas akabaki mdomo wazi huku akiendelea kumtazama Tomas aliye endelea kukigandamiza kisu hicho tumboni mwa Mac.

“T…..oo..o….ma u…me….e…ua”

“Mpelekea mtoto ndani”

Tomas alizungumza kwa ujasiri mkubwa kana kwamba hakuna kitu kilicho tokea. Tomasa hakuweza kuogopa chochote kwa maana tauari moyo wake umesha jawa na hali ya ukatili ambayo ina mfanya kufanya tukio baya kuona ni jambo la kawaida sana. Mke wa Tomas aliondoka sebleni hapo huku mwili mzima ukimtetemeka kwa woga sana. Tomas akamuachia Mac na akaanguka chini huku damu zikidi kumtoka, Tomas akafunga mlango wa mbele kwa ndani kisha akaingia jikoni na kuanza kunawa viganja vyake vilivyo jaa damu nyingi sana.

“Tom tuta fanyaje?”

Sauti ya mke wake ikamstua na kumfanya ageuke nyuma na kumtazama.

“Hoyo jamaa ana zungumza na majirani?”

“Hapana hakuna jirani anaye zungumza naye”

“Naomba simu yako”

“Una taka kufanya nini Tomas”

“Veronica wewe naomba namba simu yako”

Tomas alimuita mke waje jina lake analo lipenda. Veronica akamkabidhi Tomas simu yake, Tomas akaitafuta namba ya Ngosha na kumpigia.

“Haloo”

“Kaka ni mimi”

“Tomas, vipi mbona una zungumza na wasiwasi mwingi sana”

“Nipo kwenye matatizo”

“Matatizo gani ndugu yangu”

“Unaweza kufika hapa nilipo?”

“Niambie ni wapi?”

Tomas akamueleza Ngosha sehemu alipo kisha akamrudishia mke wake simu yake.

“Ni nani huyo jamaa?”

“Ni rafiki yangu ambaye nina ishi naye hapa Afrika kusini”

“Una muamini?”

“Ndio nina muamini, ndio maana nime muita hapa”

Baada ya nusu saa Ngosha akafika nje ya nyumba hiyo, Tomas akamfungulia na akaingia ndani. Ngosha akashangaa sana kukuta mwili wa Mac ukiwa imezungukwa na dimbwi la damu.

“Kaka nina hitaji msaada wako. Huyu ndio yule fala niliye kuwa nina kuambia kwamba ana ishi na mke wangu na hichi ndicho alicho kuwa ana kifanya kwa mke wangu katika kumpiga na kumnyanyasa kiasi hichi.”

Tomas alizugumza kwa wasiwasi huku akimtazama Ngosha usoni mwake.

“Usiwe na wasiwasi kaka. Shemeji habari yako”

“Salama”

“Huyu ana itwa Ngosha ni rafiki yangu toka nilipo kuwa sekondari”

“Nashukuru kukufahamu shemeji”

“Hata mimi nina shukuru kukufahamu shemeji. Sasa hili swala kuna mtu mwengine ana lifahamu?”

“Hapana ni sisi wawili ndio tuna lijua”

“Basi nina wapigia vijana wangu waje kusafisha hili eneo. Ila inabidi muondoke nchini ikiwezekana leo hii hii”

“Tutaelekea wapi shemeji ikiwa mume wangu nchini Tanzania ana tafuwa na sidhani kama tuna weza kwenda kwenye nchi kubwa kama Marekani kwa maana kule ulinzi wake ni mkubwa sana na wana weza kumkamata mume wangu na kumrudisha nchini Tanzania”

Veronica alizungumza huku akiwa amejawa na wasiwasi mwingi sana.

“Kuna sehemu nyingi sana duniani ambazo muna weza kwenda. Shemeji wewe jiandae kwa kwa safari”

“Sawa shemeji”

“Mtoto yupo wapi?”

“Ndani amelala”

“Sawa wewe jiandae”

Veronica akaondoka sebleni hapo na kuwaacha Tomas na Ngosha.

“Sasa kaka ilikuwaje?”

“Yaani wee acha tu. Jamaa alinivamia na kutaka kunichoma kwa kisi, katika kujilinda, nikajikuta nikikirudisha kisu hicho tumboni mwake. Je hapo nime fanya kosa?”

“Hapana hujafanya kosa ndugu yangu kwa maana ange kudhuru wewe. Ila inabidi kwa sasa muelekee nchini Nigeria, nitawasiliana na Adela aweze kuwapokea”

“Sawa ndugu yangu. Ila samahani kwa kukuingiza kwenye matatizo ambayo hakika sikuyatarajia”

“Usijali ndugu yangu mimi na wewe ni ndugu, ambao sio tu kwenye raha tuna saidiana ila hadi kwenye shida. Sasa hizi ndio shida zenyewe ndugu yangu”

“Sawa sawa nashukuru kusikia hivyo ndugu yangu”

“Poa”

Ngosha akawapigia simu vijana wake na baada ya muda mdupi wakafika eneo hilo na gari maalumu kama yanayo tumiwa na wafanya usafi kwenye majumba ya watu. Wakaingai ndani hapo kila aliye ona maiti hiyo akashangaa.

“Sasa sikilizeni. Safisheni hapa na kuwe kama hakujatokea kitu chochote”

“Sawa sawa bosi, je tuna paswa kumzika au kumdumbukiza kwenye pipa la tindikali?”

“Muingize kwenye pipa la tindikali hatuhitaji aweze kuonekana kabisa”

“Sawa”

Vijana hao wakaanza kazi ya kuuweka mwili wa Mac katika mfuko maalumu wa plastiki na kuanza kusafisha eneo hilo. Ndani ya dakika kumi na tano hapakuwa na hata alama inayo onyesha kwamba eneo hilo lilikuwa na damu. Walipo hakikisha kwamba eneo hilo lipo safi wakaondoka na mwili huo wa Mac pasipo mtu yoyote kugundua chochote.”

Veronica akatoka chumbani kwake huku akiwa amembeba mwanaye hukua kiburuza begi la nguo. Akashangaa kukuta sebeleni kwake kukiwa kumesafishwa vizuri.

“Kimetokea nini?”

“Ni kazi ya viana wangu. Umesha jiandaa kwa kila jambo”

“Ndio shemeji”

“Basi kwa sasa twendeni kwangu huku tukipanga safari ya nyinyi kuelekea nchini Nigeria”

“Nigeria?”

“Ndio shemeji. Mbona una shangaa?”

“Mmmmm ile nchi si ina makundi ya kigaidi kama Boko haramu. Mume lifikiria hilo endapo mimi na mume wangu tuta ingia kwenye matizo?”

“Tuta lizungumza hilo shemeji yangu. Ila kwa sasa twendeni kwangu”

Wakaondoka nyumbani hapo na kuianza safari ya kuelekea nyumbani kwa Ngosha.

***

Mrs Sanga alijikuta akishindwa kupata amani ya moyo wake. Kibao alicho pigwa na mume wake wala hakijamgusa moyoni mwake kama vile alivyo guswa na sauti ya Tomas.

“Una hangaika hangaika nini kitandani?”

Nabii Sanga alizungumza huku akiendelea kijitibu jeraha lake la kiganjani.

“Haikuhusu”

“Una semaje wewe?”

“Haikuhusu hujanisikia au?”

“Hivi kwa nini una kuwa na jeuri kiasi hicho. Una matatizo gani wewe mwanamke. Badala ya kujinyenyekeza mbele ya mume wako. Wewe una kazi ya kujikwenda kijinga jinga”

“Sanga una nini. Si umenipiga roho yako ime ridhika. Nini kingine unacho kihitaji zaidi kutoka kwangu, au una taka roho yangu?”

“Kama ningekuwa nina hitaji roho yako ninekuwa nimesha kutoa sadaka siku nyingi”

Kauli hiyo ikamstua sana mrs Sanga na kujikuta akikaa kitako kitandani huku akimtazama mume wake kwa sura iliyo jaa hasira.

“Kwahiyo ulihitaji kunitoa sadaka?”

“Siwezi kukutoa sadaka ila kuna mtu nina hitaji kumtoa sadaka”

“Wewe toa sadaka watu wote, ila si wanangu. Haki ya Mungu mwanangu yoyote akifa nita hakikisha kwamba dunia nzima ina fahamu ukatili wako na hakuna utumishi wowote ndani yako”

“Yaani siku utakayao fungua kinywa chako ndio siku ambayo dunia ita mpata nguruwe mwenye kichwa cha mtu. Tena atakuwa na kicha chako wewe.”

Nabii Sanga mara baada ya kuzungumza hivyo akafaunga kiboksi hicho chenye vifaa vya huduma ya kwanza.

“Alafu jambo jengine ni kwamba. Usidhubutu kunitishia kwamba una zungumza siri zangu. Wewe zungumza na uta nitambua vizuri mimi ni nani”

Nabii Sanga alizungumza kwa msisitizo na kumfanya mrs Sanga kunywea kidogo.

“Tenda tuondoke muda huu. Tunarudi Tanzania”

“Eheee!!?”

“Tuna rudi nchini Tanzania, kaoge ubadilishe nguo zako”

“Jamani nimechoka kusafiri safiri kwenye mandege mimi”

“Ndio hivyo. Oga safari ya Tanzania ime wadia na sasa hivi ni saa mbili asubihi hivyo by saa tano tutakuwa tumepata ndege ya kurudi nchini Tanzania.”

Kutokana nabii Sanga ndio msemaji wa mwisho, mrs Sanga hakuwa na kipingamizi chochote zaidi ya kufwata amri ya mume wake ya kujiandaa kwa ajili ya kurudi nchini Tanzania.

***

“Mage tunasubiria jibu lako”

Vivian alizungumza huku akimtazama Magreth usoni mwake.

“Ninaomba munipatie muda. Inabidi nijadiliane na mume wangu katika hii. Nipeni siku ya leo kisha kisho muta lipata jibu lenu”

“Sawa ni wewe tu, jambo kubwa tuna tarajia kupata majibu mazuri kutoka kwako”

“Musijali nina heshimu uchaguzi wenu wa kunichagua mimi”

“Sawa Magreth nikutakie kazi njema na siku njema kwa ujumla”

“Nawe pia mzee”

Magreth akatoka ofisini hapo na Viviana.

“Mage hakika hii ni bahati ya kipekee ambayo ume ipata. Huwa mara kadhaa tuna fanya matangazo na wasanii wakubwa wa filamau na wasanii wa muziki, ila kwa kweli matangazo hayo huwa hayatulipi sana kama vile tunavyo tarajia”

“Ila ni kitu gani ambacho mume kiona kwangu. Ikiwa mimi sio maarufu na biashara yangu ndio kwanza ina anza?”

“Kuna mambo mengi sana ambayo tumeyaona kwako. Kimojawa wapo ni nguvu ya ushawishi. Unajua mimi ni mtu wa kukosoa kosoa vyakula ila nilipo kula chakula chako na marafiki zangu, tulijikuta tukihitaji kula tena na tena. Kiufupi upo vizuri madam Magreth”

“Hahaa nashukuru sana dada Vivian”

Wakafika hadi kwenye maegesho ya magari. Wakaagana na Magreth akaingia kwenye gari lake na kurudi kazini kwake. Akamkuta bi Ngedere akiwa bado ana msubiri.

“Mage mgahawa wako una watu wengi”

Bi Ngedere alizungumza huku akiachia tabasamu la kinafki ila moyoni mwake amejawa na wivu mkubwa sana.

“Mungu ana bariki, ehee ume onaje chai ya hapo?”

“Ni nzuri na tamu”

“Eti ehee?”

“Ndio”

“Boss samahani nina weza kuzungumza na wewe?”

“Ndio tuna weza kuzungumza”

Magreth akasimama na kumfwata Juma sehemu alipo simama.

“Kuna jambo kidogo ambalo nina omba nikushirikishe kama huto jali”

“Zungumza tu Juma”

“Huyu mama ni nani yako?”

“Alikuwa ni mama mwenye nyumba yangu huko uswahilini nilipo kuwa ina ishi.”

“Hivyo bado una mazoea naye mazuri?”

“Kivipi?”

“Yaani una muheshimu kama mama yako au?”

“Mmmm kiasi niambie kuna nini?”

“Mama huyu ni mchawi na hapa alipo ana jitahidi sana kuhakikisha ana fanya kila linalo wezekana ana wafukuaza wateja wetu kwa nguvu zake za kichwawi.”

Kauli hiyo kidogo ikamstua Magreth.

“Juma wewe ume juaje!!?”

“Mimi nimezaliwa Tanga na babu yangu ni mganga. Kichwani mwangu nina majini hivyo mtu akiwa ni mbaya basi huwa nina fahamu kwamba huyu mtu ni mbaya na hiyo shida ya laki tatu ambayo ana hiyaji tafadhali usimpatie kwa mkono wake, kama ina wezekana umtumie kwenye simu yako”

“Juma hayo yote ume yajuaje kama ana shida ya laki tatu”

“Boss nimekuambia kwamba mimi nime tokea Tanga na nina majini ambayo hakika yana uwezo wa kumjua mtu mbaya. Kama huamini ngoja nikuonyeshe uchawi wa huyo bibi hapo”

“Una nionyeshaje Juma”

Magreth alizungumza huku akiwa ana zidi kushangaa kwa kila jambo analo ambiwa na kijana huyo. Juma akamshika mkono Magreth na wakatembea hadi kwenye meza aliyo kaa bi Ngedere peke yake.

“Bibi uta endelea na mpango wako wa kuhitaji kutufukuzia wateja au nikuumbue kwa kila mtu kwamba wewe ni mchawi?”

Kauli hiyo ikamstua san bi Ngedere na kumfanya mapigo yake ya moyo kuanza kumuenda kasi huku mwili mzima ukianza kumtetemeka kwa woga hadi Magreth akaanza kuhisi alicho kizungumza Juma ni jambo la ukweli kabisa kwani si kwahali hiyo inayo endelea kwa bi Ngedere.



“U…naa….na….zu…ng…umzia nini wewe?”

Bi Ngedere alizungumza huku midomo yake yote ikimtetemeka kwa woga. Juma akamshika mkono wake wa kulia na kuuvuta karibu. Kitendo hicho kimfanya Bi Ngere kuurudisha nyuma mkono wake kwa haraka na kumfanya Magreth kushangaa.

“Mage umenileta hapa ili kunidhalilisha au?”

Bi Ngere alizungumza kwa ukali huku akimtazama Magreth na Juma wanao endelea kumkodolea macho. Juma akaushika tena mkono wa kulia wa bi Ngerede na safari hii Juma hakuhitaji kuuachia japo bi Ngedere ana hitaji kuurudisha nyuma. Juma kwa kutumia nguvu zake, akafungua kiganja cha mkono huo wa kulia wa bi Ngedere. Magreth macho yakamtoka kwani iridhi kubwa ya rengi nyeusi inayo pumua mithili ya moyo wa binadamu, ndio ina onekana mkononi mwa bi Ngedere.

“Bosi ume ona?”

Bi Ngedere mwili mzima ukaizidi kumtetemeka kwa woga. Magreth akamtazama bi Ngedere kwa macho yaliyo jaa hasira kali sana.

“Hichi ndio kitu nilicho kuambia”

“Bi Ngedere kwa usalama wako, nifwate la sivyo watu wote hapa kwenye huu mgahawa watajua kwamba wewe nimchawi. Si unajua jinsi gani Dar es Salaama wachawi wanavyo fanywa. Sasa wewe nifwate”

Bi Ngedere machozi yakaanza kumlenga lenga, mipango yake yote ime mvurugika. Akanyanyuka na kuanza kumfwata Magreth aliye tangulia mbele huku Juma akiwa ana mfwata kwa nyuma. Wakaingia katika chumba kinacho tumika kama jiko na upende huo ni wapishi na wafanyakazi wa mgahawa huo ndio wana paswa kuingia.

Magreth akamzaba bi Ngedere kibao cha uso na kuwafanya wapishi wawili waliomo ndani ya chumba hicho kushangaa kwa maana hawaelewi ni kitu gani ambacho kina endelea.

“Mwanamke mpumbavu kweli wewe. Unahisi kwamba una weza kunirudisha kwenye umasikini wa kutembeza maandazi kama pale awali eheee?”

Magreth alizungumza kwa hasira sana huku akimtazama bi Ngedere anaye zidi kutetemeka huku machozi yakimtoka.

“Bosi kuna nini?”

“Huyu bibi ni mchawi, amekuja hapa mgaawani kwangua kiwa na muirizi wake hapo. Juma waonyeshe”

Juma akakunjua kiganja cha mkono wa kulia wa bi Ngedere ambao umeshika irizi hiyo. Wapishi hao wawili wakabaki wakiwa wamejawa na mshangao mkubwa sana. Mpishi mmoja akachukua kishoka maalumu cha kukatia nyama na kutaka kumpiga nacho kichwani bi Ngedere ila Juma akamzuia.

“Acha hatutaki kumwaga damu ya wachawi hapa kwenye mgahawa.”

Juma alizungumza huku akimzuia jamaa huyo.

“Mchawi na mwizi siku zote sio watu wa kuishi. Wana rudisha maendeleo ya watu nyuma. Acha tumcharange, hivi dada Mange leo hii akifulia sisi tutakwenda kuishi maisha gani ehheee?”

“Hussein tulia, huyu tuna malizana naye”

Magreth alizungumza kwa msisitizo huku akiendelea kumkazia macho bi Ngedere.

“Ndio maana siku zote wapangaji wako hawaendelei kwenye ile nyumba. Laiti kama nisinge kuwa na Mungu ndani yangu, ningekuwa nina uza maandazi hadi leo si ndio?”

Magreth alizungumza kwa hasira sana huku machozi yakimlenga lenga. Siku zote alihisi tatizo kubwa la bi Ngedere ni mdomo wa kuropoka ropoka mambo, kumbe yupo hadi kwneye mambo ya kishirikina. Magreth akamtandika bi Ngedere kofi jengine hadi iridhi aliyo ishika ikaanguka.

“Ahaa…..kum***k*** walai. Dude lina pumua”

Hussein alizungumza huku akishangaa iridhi hiyo jinsi inavyo puma hapo ilipo angukia.

“Una kazi ya kuwaweka wapangaji wa watu katika wakati mgumu, wana fanya biashara ila hawatoki. Waume zao kila asubuhi wana kasi ya kudimka kuwahi makazini ili wapate miambili mia tatu kumbe wewe malaya mzee una wachawia. Sasa leo nina kwenda kukuadhirisha mbele ya wapangaji wako”

“Aha….Mage nakuomba usinifanyie hivyo mwanangu”

“Koma wewe mimi sio mwanao. Unajua uchungu wangu wewe. Ungekuwa ni mwanamke unaye jiheshimu unge nitakia mema. Yaani umeona nime fanikiwa kidogo una kuja kuniroga hadi hapa. Yaani jamani hivi waswahili sisi tupo vipi jamani”

Magreth alizungumza kwa uchungu sana huku machozi yakimwagika usoni mwake.

“Okota dude lako”

Magreth alizidi kufoka huku akitamani kumvamia bi Ngedere na kumpa mangumi ila ana jiheshimu na kuheshimu eneo lake la kazi. Bi Ngedere akaokota irdhi yake huku aibu kubwa ikiendelea kumtafuna taratibu.

“Juma hakikisha ana fika kwenye gari langu. Tuna kwenda nyumbani kwake sasa hivi”

“Sawa bosi”

“Mage Mage, tuyaongee mwanangu”

“Nyamaza wewe nita KUUAAAAAA”

Magreth alizungumza huku macho yakimtoka. Kila mtu akashangaa kumuona Magreth kwenye hali kama hiyo, uzuri wake wote ume potea na amekuwa ni mtu wa tofauti sana.

“Mama hujui kabila langu wewe. Nitakuuaa Juma mtoea hapa”

“Sawa mkuu”

“Tena ingia naye kwenye gari nina kuja”

Magreth alizunguumza huku akimkabidhi Juma funguo za gari lake. Juma na bi Ngedere wakatoka jikoni humo huku Juma akiwa amemshika bi Ngedere mkono. Magreth akapiga piga makofi ukutani kuipunguza hasira yake.

‘Ohoo Mungu nisaidie’

Magreth alizungumza kimoyo moyo huku akiinama. Akavuta pumzi ya kutosha, kisha akasimama wima huku akiwatazama wapishi wake hao ambao ana shirikiana nao katika maswala ya kupika.

“Hakikisheni kwamba chakula kina kuwa kizuri kama vile ninavyo hitaji siku zote”

“Usijali bosi”

“Haya yaliyo tokea humu ndani iwe siri yenu. Sitaki kuyasikia kwa hawa wadada au mtu mwengine mume nielewa?

“Usijali bosi hatuwezi kumueleza mtu yoyote. Ila pole sana”

“Asante Hussein”

Magreth akajiweka uso wake vizuri na kufuta machozi yote. Akatoka ndani humu na kuwakuta wahudumu wake wa kike wakiendelea kuwahudumia watu vizuri.

“Nina toka nitarudi baada ya muda kidogo”

Magreth aliwaambia wafanyakazi wake hao, kisha akeleeka kwenye maegesho ya magari na kuwakuta Juma na bi Ngedere wakiwa wamekaa siti ya nyuma. Magreth akaka kwenye siti yake huku akishusha pumzi, akajifunga mkanda huku akitafakari kidogo.

“Juma mzigo wkae huyo si anaoa?”

“Ndio bosi”

“Hakikishi haitupi ndani ya gari langu na tusije tuka pata ajali”

“Hawezi bosi hapa nilipo nime mamkamaya kisawa sawa.”

“Poa”

Magreth akawasha gari na wakaondoka eneo hilo na kuianza safari ya kuelekea nyumbani kwa bi Ngedere ili akamuumbue kwa wapangaji wake.

***

Nabii Sanga na mke wake wakarudisha funguo katika hoteli hiyo japo walipanga kukaa hotelini hapo kwa siku saba.

“Vipi muheshimiwa, mbona muna ondoka mapema. Kuna tatizo lolote kwenye huduma za hoteli yetu?”

Muhudumu aliuliza kwa mshangao kwa maana watu hao wame ingia asubuhi hiyo na wanaondoka asubuhi hiyo hiyo.

“Hapana vyumba vyenu vipo vizuri na hakika tumevipenda. Ila kuna dharura ime tokea hivyo ina tupasa kuondoka”

Nabii Sanga alizungumza huku akiwa amejawa na tabasamu pana sana usoni mwake. Ila mke wake dhahiri ana onekana haja penda kuondoka muda huo.

“Ahaa karibuni sana”

“Tunashukuru”

Wakababe mabegi yao hadi nje, wakakodisha taksi na kumuomba dereva huyo waelekee kwenye maduka.

“Tuna kwenda kufanya nini huko?”

Mrs Sanga aliuliza huku macho yakiwa yamemtoka.

“Dereva wewe twende”

Nabii Sanga alizungumza pasipo kujali swali la mke wake. Wakafika katika mtaa wenye maduka mengi sana.

“Mimi sishuki nime choka na nina usingizi. Nita kusubiria humu ndani ya gari”

“Utajijua mwenyewe”

Nabii Sanga alizungumza huku akishuka kwenye gari. Akaingia kwenye moja ya duka linalo uza vito vya dhahabu, akaanza kuangaza angaza huku na kule huku akimtafutia Magreth mkufu mzdhuri wa garama.

“Ah…huu mkufu ni kiasi gani?”

“Ni dola elfu kumi na tano”

“Sawa je huu hapa?”

Nabii Sanga alionyesha mkufu mwengine ulio pambwa na madini mbalimbali.

“Huu hapa ni dola elfu stini mkuu”

“Okay nipatie huu, si ninapata na herini zake?”

“Ndio bosi”

Muhudumu huyo alizungumza huku akiwa amejawa na furaha sana kwani ni watu wachache sana huwa wana wanunulia wapenzi wao mikufu yenye thamani kubwa kama huo.

“Nipatie miwili inayo fanana na hiyo”

“Sawa muheshimiwa”

“Itenganishe, kila mmoja uwe kivyake. Mmoja niwekee kwenye mfuko na mwengine nipe tu katika kisanduku chake”

“Sawa sawa muheshimiwa”

Nabii Sanga akaendelea kuangaza mapambo hayo ya thamani kwa ajili ya wanawake. Akaona pete nzuri sana iliyo tengenezwa kwa madini ya diamond.

“Kijana hii ni dola ngapi?”

“Dola elfu kumi mkuu”

“Nipatie hii pete”

Kijana huyo kwa haraka akaitoa pete hiyo, nabii Sanga akaitazama kwa sekunde kadhaa na kutingisha kichwa akiamini kwamba inatosha kabisa kuingia kidoleni mwa Magreth. Nabii Sanga akaendelea kuangaza huku na kule akiendelea kutafufa zawadi za garama kwa Magreth na mwanaye.

“Hii saa hapa je?”

Nabii Sanga alionyesha saa iliyo tengenezwa kwa madini ya dhahabu tupu.

“Hii ni dola elfu ishirini na tano”

“Naomba mbili”

Muhudumu huyo akatoa saa hiyo huku akiona ni habati kubwa sana kwa kupata mteja kama huyo asubuhi asubuhi hiyo.

“Kuna wanaume wana kera sana”

Mrs Sanga alizungumza hukua akiachia msunyo mkali sana. Gari nyeusi aina ya RANGE ROVER VOG ikapaki mbele ya taksi hiyo, akashuka jamaa mmoja mweusi kiasi na mrefu na akaanza kutembea kuelekea kwenye duka hilo.

***

“Jamani kabla hatujaenda nyumbani kwangu. Tupitie madukani kidogo ili tununue baadhi ya nguo kwa ajili yenu”

Ngosha alitoa wazo hilo na Tomas pamoja na mke wake wakaliunga mkono. Wakafika kwenye baadhi ya maduka na kununua nguo, viatu pamoja na mahitaji ya Veronica.

“Kuna duka langu moja lipo mtaa wa pili hapo nina udha vito vito vya thamani kwa ajili ya wanawake. Tupiteni hapo nikamchukulie shemeji japo mkufu”

“Sawa kaka”

Ngosha akawasha gari lake hilo aina ya Range rover Vog, Hawakumaliza hata dakika tano wakafika dukani hapo, akasimamisha gari lake mbele ya taksi aliyo ikuta ime simama mbele ya duka lake.

“Kaka humu hakuna bidhaa za kiume vipi una shuka au niende kumchagulia shemeji mkufu nilio ahidi kumpatia?”

Tomas akajibu kwa ishara ya kidole akimuonyeshea mwanaye aliye mbeba huku akiwa amemlaza kifuani mwake.

“Kweli bwana mkubwa ame lala. Basi ngoja nishuke, au shemeji una hitaji tukachague ndani?”

“Mmmm hapana shemeji, unajua hiyo ni zawadi, sasa nikiwanina hitaji kuchagua ninacho kihitaji nitakutia hasara bure”

“Hahaa hapana huwezi ninipa hasara”

“Nashukuru sana shemeji, acha sisi tukusubirie humu”

Ngosha akashuka kwenye gari hilo na kuingia dukani kwake na kumkuta mfanyakazi wake akiwa bize na mteja mmoja.

“Hei vipi Poul”

“Safi sana bosi karibu”

“Nashukuru, biashara ina kwendaje?”

“Safi sana bosi yaani yule mzee pale hadi sasa hivi ame nunua vitu vinavyo karibia dola laki mbili”

“Wewee!!”

“Ndio bosi yaani asubuhi ya leo ime anza vizuri sana”

“Mambo yakiwa vizuri, ikifika mida fulani wewe funga duka kapumzike na katika mauzo ya leo utachukua asilimia tano sawa”

“Nashukuru sana bosi”

Ngosha akaanza kuzunguka zunguka kwenye dula lake hilo kubwa ambalo lina vitu vingi sana vya thamani. Japo duka ni kubwa ila ameamua kuwa na muuzaji mmoja tu kwani Poul ni mchapakazi na ni mtu muaminifu sana.

“Rafiki yako ana onekana ni mkarimu sana?”

Veronica alimuuliza Tomas huku akimtazama usoni mwake.

“Yaa jinsi alivyo hapa ndivyo jinsi alivyo kuwa shuleni. Ana roho nzuri sana”

Mlio wa simu ya Ngosha alio iacha kwenye siti ya mbele katika gari hilo ikawafanya Tomas na Veronica kutazamana kwa sekunde kadhaa.

“Mpelekee simu ina weza kuwa ya maana”

“Hapana Tomas hiyo ni simu ya mwanaume mwenzako. Mimi siwezi ishika, mlete mtoto umpelekee”

Tomas akamkabidhi Magreth mtoto, kisha akaichukua simu hiyo, akafungua mlango wa gari hilo na kushuka. Akaanza kuelekea ndani ya duka hilo. Moyo wa mrs Sanga ukalipuka kwa mstuko mkubwa sana mara baada ya kumuona Tomas akielekea ndani ya duka hilo huku akiwa katika hatua za haraka ambazo zina onyesha dhairi kuna mtu ana mfwata ndani ya duka hilo na mtu wa pekee ambaye mrs Sanga ana mfikiria akilini mwake ni mume wake kwani yeye ndio mwenye bifu kubwa na Tomas na alishuhudia unyama ambao nabii Sanga alimfanyia Tomas.



Mrs Sanga akataka kutoka ndani ya taksi hiyo ila kabla hajafungua mlango, akamshuhudia mwanaume ambaye alimuona akiingia dukani humo, akitoka na wakakutana na Tomas mlangoni. Akashuhudia Tomas akimkabidhi mwanaume huyo simu, kisha Tomas akarudi ndani ya gari. Ngosha akamaliza kuzungumza na simu hiyo na kurudi ndani ya gari.

“Shemeji vipi huu mkufu ume upenda?”

Ngosha alizungumza huku akimuonyesha Victoria mkufu huo.

“Waooo asante sana shemeji, nimeupenda”

“Nashukuru kwa kushukuru. Sasa turudini nyumbani”

Ngosha alizungumza, akawasha gari na wakaondoka eneo hilo. Mrs Sanga akashusha pumzi huku wasiwasi ukitulia kwani hakujua ni kitu gani kingetokea kama nabii Sanga angekuatana uso kwa Tomas. Baada ya nabii Sanga kumaliza kununa kila alicho kihitaji akarudi kwenye taksi hiyo.

“Zawadi yako”

Nabii Sanga alizungumza huku akiweka boksi maalumu lililo na cheni juu ya mapaja ya mrs Sanga.

“Eheee”

“Zawadi yako una stuka stuka nini?”

Nabii Sanga alizungumza huku akiwa amejawa na jazba kidogo. Mrs Sanga akachukua kiboksi hicho chenye rangi nyekundu na kuifungua. Akakuta cheni nzuri ya dhahabu.

“Asante”

Mrs Sanga alizungumza huku akiendelea kumuwaza Tomas. Nabii Sanga akamkata mke wake jicho la hasira, kwani kwa zawadi ya aina hiyo hakutakiwa kujibu kwa ufupi namna hiyo. Safari ya kuelekea uwanjani wa ndege ikaanza na hawakuchukua muda mrefu sana wakafika uwanjani hapo. Wakakaa kwa nusu saa kisha wakaingia kwenye ndege na safari ya kuelekea nchini Tanzania ikaanza.

***

Magreth akasimamisha gari lake mbele ya nyumba ya bi Ngedere. Akamkuta baba bakari akiwa ana kanga mihogo kibarazani hapo huku akiwa amezungukwa na wateja kadhaa.

“Mage tafadhali nina kuomba usinifanyie hivyo”

Bi Ngedere aliomba kwa unyeyekevu huku akimtazama Magreth aliye kaa siti ya mbele.

“Mama mimi sirogeki kijinga. Yaani nilikuacha pale kwa lengo zuri sana ila mwisho wa siku una nifanyia mambo ya ajabu”

Magreth alizungumza kwa msisitozo huku akimtazama bi Ngedere aliye keti siti ya nyuma. Magreth akafungua mlango wa gari lake na kushuka. Mama Boka na wateja wote wanao mtambua Magreth wakabaki wakiwa wamejawa na mshangao. Kwani Magreth yule waliye kuwa wana mfahamu, amebadilika sana. Magreth amekuwa ni mzuri kupita maelezo. Juma akamfungulia bi Ngedere na kwa ishara ya macho akamuomba ashuke. Taratibu bi Ngedere akashuka huku mwili mzima ukimtetemeka. Juma naye akashuka kwenye gari huku akiwa amesimama karibu kabisa na bi Ngedere.

“Mage”

Mama Boka alizungumza huku akimtazama Magreth.

“Ndio mimi shosti yangu”

“Waooooo”

Mama Boka alizungumza huku akiacha shuhuli ya kuwahudumia wateja wake hao. Akakumbatiana na Magreth kwa furaha kwani ni shosti yake wa kipindi kirefu sana.

“Shosti yangu ume badilika jamani”

“Mungu ana bariki bariki. Niambie una endeleaje?”

“Kama unavyo ona. Jinsi ulivyo tuacha ndivyo jinsi ulivyo tukuta”

“Watu wote wapo?”

“Ndio wapo, hawajaamka wengine”

“Kama huto jali nina kuomba uwaamshe. Nahitaji kuzungumza nao hapo kwenye kordo”

“Kuna nini?”

“Wewe nakuomba ufanye hivyo mama Bakari”

“Sawa hakuna tatizo. Wewe Asha niangalizie mihogo yangu isiungue”

Mama Boka akaanza kuingia ndani, huku Magreth, bi Ngedere na Juma wakimfwata kwa nyuma. Magreth akafunga mlango huo wa mbele, kisha akapitiliza hadi katika mlango wa uwani. Akachungulia kwa nje ili kuona kama kuna mtu ana pika uwani hapo, ila hakumuona. Akafunga mlango huo na kusikama kwenye kordo hiyo. Wapangaji wote wakatoka vyumbani kwao huku wengine wakitoka na waume zao. Kila mmoja akamsalimia Magreth kwa furaha sana, kwani katika kipindi chote cha miaka zaidi ya minne wame ishi naye kwa amani na upendo.

“Jamani kwanza nina waomba munisamehe kwa kuwaamsha muda na wakati kama huu”

“Bila msahama tulikuwa tumesha amka”

“Jamani nimekuja na jambo moja muhimu sana ambalo niliona nisipo fanya kama hivi basi nyinyii wengine nitakuwa nime waacha katika wakati mgumu na mateso mazito sana. Ila kabla sija zungumza mimi, bi Ngedere zungumza kile ulicho kifanya leo ufisini kwangu”

Bi Ngedere mwili mzima ukaanza kumtetemeka, siku zote amezoelekea kuwa mzungumzaji mkubwa snaa ila watu wote wakashangaa kumuona akiwa amejawa na kigugumizi na kushindwa kuzungumza kabisa.”

“Zungumza wewe mama, au una taka nikushushushie makofi”

Magreth alizungumza kwa ukali kidogo ulio zidi kuwashangaza wapangaji wengine kwani siku zote wamesha zoea kumuona Magreth akiwa ni mpole na mnyenyekevu.

“Shosti yangu kuna nini kinacho endelea?”

“Mama Asha wewe ngoja, atazungumza yeye mwenyewe. Uzinipotezee muda zungumza”

“Mimi…leo…leo ni..li…li ku…tana na….na Mage ku…ku…le….le….”

“Mbona ume jawa na kigugumizi. Juma hembu waonyeshe”

Juma akaushika mkono wa kulia wa bi Ngedere na kuvifungua kwa nguvu viganja vya mkono huo. Wapangaji wote wakajwa na mshangao mara baada ya kuona iridhi kubwa inayo pumua kwenye kiganja cha bi Ngedere.

“Sikuzote tumekuwa tukiishia hapa kwenye hii nyumba na kukubaliana na manyanyaso ya huyu mama. Ila ukweli ni kwamba ni mchawi. Leo asubuhi nilimuacha kwenye mgahawa wangu mpya. Ila kwakutumia iridhi yake sijui alikuwa na mpango wa kuwafukuza wateja wangu, au alikuwa na mpango wa kuzorotesha biashara yangu.”

Wapangaji wakazidi kujawa na mshangao.

“Huyu mwana mama amekuwa akitumia njia hii kutudhohofisha kimaendeleo na kiuchumi. Ona ndani ya miaka yote tulio kaa hapa ni kipi cha maana tulikifanya chini ya utawala wa huyu mama?”

Magreth aliendelea kuzungumza kwa jazba.

“Zungumza ni kitu gani ulicho kuwa una tufanyia”

“Jamanii wee mama kumbe ni mwanga kiasi hicho.”

Mama Boka alizungumza huku akimtazama kwa kejeli bi Ngedere anaye mwagikwa na machozi.

“Ni nani na nani ambaye ume mfanyia ubaya humu ndani?”

“Ni…niii….wapangaji wote”

“Heeeee”

Karibia wanamama wote walihamaki, huku kila mmoja akiwa amejawa na maswali ni kitu gani ambacho amefanyiwa na bi Ngedere.

“Zungumza ni kitu gani ambacho umefanyia kila mpangaji wako?”

Bi Ngedere akaanza kuwatazama wapangaji wake mmoja baada ya mwengine.

“Mama boka huwa nina….nina gawana naye kila anapo uza mihogo yake”

“Wee wee weee weee weeee mama. Kumbe ni kopera ehee?”

Mama Boka alizungumza huku akijifunga vizuri tenge lake vizuri, akataka kumvamia bi Ngedere ila mume wake akamzuia.

“Baba boka acha nimfundishe adabu mwanga mkubwa huyo. Mimi nina pambana kila asubuhi kupata vimia mbili mia tatu ila ana niletea using** wake mimi”

Mama Boka alizidi kufoka.

“Mama Boka tulia, zungumza mwengine”

Magreth alizungumza huku akimkazia macho bi Ngedere.

“Huwa….ni…nina lala na baba Asha kila siku usiku, nina ingia chumbani kwake kimazingara na kulala naye”

Mama Asha akajikuta akikaa chini huku akihisi presha ikishuka. Baba Asha uso ukamjaa mikunjo ya hasira, ila kutokana bado wapangaji wawili hajawaelezea ni kitu gani ambacho ame wafanyia ikamlazimu kutuliza hasira zake.

“Endelea”

Magreth aliendelea kumsisitizia bi Ngedere.

“Huwa nina tumia nyota ya mtoto wa mama Omary kwenye mambo yangu ya kichawi”

“Kum….ko wewe mama. Una mroga mwanangu”

Baba Omary alishindwa kujizuia na kujikuta akimvaa bi Ngedere na akaanguka chini. Akaanza kumtandika makofi mazito na kumfanya Juma kuamua ugomvi huo.

“Mutaniua jamani”

“Kufa mbwa wewee”

Mama Omary naye alizungumza huku akimtandika kwa lapa bi Ngedere. Vurumai la wapangaji hao wanao mshambulia bi Ngedere, likazidi kila mpangaji akazidi kushindwa kuzuia hasira yake. Juma akajitahidi kumtoa bi Ngedere mikononi mwa wapangaji wake na kumuingiza chumbani kwake.

“Wewe mama leo lazima tukuue”

Baba Omary alizungumza huku akiwa amefura kwa hasira. Bi Ngerere akaona hata kukuaa chumbani kwake hapo itakuwa ni shida. Akaingia chini ya kitanda chake huku akiendelea kutetemeka kwa woga mkubwa sana.

“Jamani naombeni tutulize jazba. Ninajua mimi ndio niliye mleta hapa nyumbani huyu bibi. Ila jambo moja la msingi ambalo nina hitaji kuwaomba, kila mtu apambane na hali yake. Endapo ataamua kufanya mambo yake usiku basi tambueni kwamba hato kuja kirafiki”

Magreth alizungumza kwa msisitizo.

“Hato weza kufanya hivyo”

Juma alimkatisha Magreth.

“Kwa nini?”

“Iridhi yake hii ndio kiungo kikubwa katika utendaji wa kazi wake. Akiiamerisha hii iridhi kufanya jambo basi ina fanya. Tukiichoma moto basi kila kitu kitakwenda kumuishia”

Juma alizungumza huku akiwa ameishika iridhi hiyo.

“Kuna mafuta ya taa”

Baba Omary alizungumza huku akiingia chumbani mwake, akatoka akiwa ameshika kidungu cha mafuta ya taa. Wakaelekea nyuma ya nyumba hiyo na kuichoma iridhi hiyo na ikaanza kuruka ruka mithili ya kuku aliye chinjwa na kuachiwa pasipo kukata roho vizuri.

“Jamani huyu bibi ni mwanga ehee? Hadi iridhi zina ruka ruka namna hiyo”

“Ndio hiyo. Ila jamani mimi ndio niliye mvumbua huyo bibi. Sinto pendelea muendelee kumshambulia kwa kumpiga. Amefanya makosa tafadhali, musi mdhuru kwa maana kufanya hivyo wezake ambao wame ungana na yeye wata kwenda kuwadhuru na si kuwadhuru kwa hali ya kawaida tu, ila hata muta weza kupoteza uhai wenu au wa watoto wenu”

Juma alizungumza kwa msisitizo huku akiwatazama wapangaji hao.

“Ila kaka si ume sema kwamba tukiichoma hii iridhi kila kitu kita kuwa kime kwisha?”

“Kwisha ndio kitakuwa kime kwisha. Ila je wezake ambao wana muunga mkono kwenye kilinge chao, je wata waacha?”

Kila mpangaji akaanza kuingiwa na wasiwasi.

“Kuweni makini kwa maana mume anzisha vita ambayo sinto penda mupambane nayo kwa maana ita wagarimu sana. Bosi nime kamilisha kazi yangu, nitakusubiria nje”

Juma akaondoka eneo hilo na kumuacha Magreth na wapagaji wa bi Ngedere wakiwa katika hali ya sinto fahamu.

“Jamani leo kidogo ratiba yangu ime nibana ila nitaomba nije weekend hii niwape michongo ya kibiashara ili kila mmoja aweze kutoka kimaisha”

“Sawa Mage”

Magreth akaondoka eneo hilo, akaingia kwenye gari lake na wakarudi ofisini na Juma.

***

Majira ya saa moja usiku, nabii Sanga na mke wake wakafika nchini Tanzania. Wakapokelewa na Julieth waliye wasiliana naye kwamba wana rudi siku hiyo. Baada ya kusalimiana kwa furaha nabii Sanga akamkabidhi Julieth mfuko wenye zawadi zake.

“Nyinyi tangulieni nyumbani”

Nabii Sanga alizungumza mara baada ya mke wake na mwanaye kuingia ndani ya gari.

“Kwa nini baba”

“Kuna mahala nina elekea baada ya hapo nitarudi nyumbani”

“Sawa baba”

Mrs Sanga akamtazama mume wake huku akimtilia mashaka mengi sana kisha kwa ishara akamruhusu mwanaye kuondoa gari hilo. Nabii Sanga akatafuta taksi ya kukodi na kumuomba impeleke eneo ambalo upo mgahawa wa Magreth.

“Julieth simamisha gari”

“Kwa nini mama?”

“Nahitaji tuifwatilie taksi aliyo panda baba yako. Hembu bana hapo pembeni”

Julieth akafanya vile alivyo agizwa na mama yake. Taksi aliyo panda nabii Sanga ikawapita pasipo nabii Sanga kuliona gari hilo la binti yake.

“Haya sasa ifwatilie taksi ya ile hakikisha kwamba baba yako hatambui kama tuna ifwatilia taksi hiyo?”

“Ila kwa nini mama tuna fanya haya yote?”

“Julieth fanya kama nilivyo kuambia sihitaji maswali mengi”

Mrs Sanga alizugumza huku akiwa amejawa na hasira moyoni mwake. Kwani toka walipo kuwa Afrika kusini hapakuwa na amani yoyote kati yake na mume wake.


Julieth akaendelea kuifwatilia taksi hiyo ila kadri jinsi anavyo mtazama mama yake usoni, ana ona dhairi kwamba kuuna tatizo linalo endelea kati ya baba na mama yake.

“Mama una weza kunishirikisha ni kitu gani ambacho kina endelea kati yenu nyinyi wawili”

“Mwanangu kichwa changu hakipo sawa. Ila usiipoteze hiyo taksi”

“Sawa”

Julieth alijibu kwa unyonge huku akiendelea kuifwata kwa nyuma taksi hiyo. Wakaishuhudia taksi hiyo ikisimama kwenye mgahawa mkubwa sana ulio jaa wateja.

“Sasa mama baba hapa si atakuwa amekuja kununua chakula”

“Hapana kuna mtu amekuja kuonana naye hapa. Tusubiri kuona ni nani”

Mrs Sanga alizungumza huku hasira ya wivu ikianza kumtawala moyoni mwake. Nabii Sanga akatazama jinsi watu wengi walivyo jaa katika mgahawa huo. Uwepo wake katika mgahawa huo una weza kuwafanya wateja hao kumzonga zonga kwa maana ni nabii mwenye wafuasi wengi sana ndani ya Tanzania.

“Kijana nina kuomba unisaidie jambo moja”

“Ndio”

“Kuna binti ana itwa Magreth ndio mmiliki wa huu mgahawa. Nenda ukamuulize na nina kuomba ukamuite”

“Sawa, nimuambie ana itwa na nani?”

“Mwambie kuna mgeni wake muhimu sana ana muita”

“Sawa”

Dereva wa taksi akashuka na kumuuliza mmoja wa wahudumu wa mgahawa wa Magreth.

“Bosi yule pale, aliye simama na wale wadada wawili”

“Nashukuru”

Dereva taksi akamfwata Magreth aliye simama na wateja wake wawili.

“Samahani dada nina maagizo yako”

“Bila samahani, ila unaweza nipa japo dakika moja nikamalizana na hawa wateja wangu”

“Hakuna shaka”

Dereva huyo akasogea pembeni na kumpa nafasi Magreth kumaliza kuzungumza na wateja wake. Baada Magreth kumaliza kuzungumza na wateja hao, akamsogelea dereva taksi huyo.

“Samahani kwa kukuchelewesha kaka yangu”

“Hakuna tatizo. Ila kuna mgeni wako ndani ya taksi yangu ana kusubiria”

“Mgeni wangu muhimu, ametokea wapi?”

“Hakika sifahamu ila nilimchukua na gari yangu kutokea uwanja wa ndege. Hivyo kama huto jali una weza kuzungumza naye.”

Magreth akamtazama kijana huyo, kwa muonekanao wake anaonyesha kwamba hana uwovu ndani yake.

“Sawa twende tukamuone”

Wakatembea kwa pamoja hadi kwenye taksi hiyo, taratibu kioo cha nyuma cha gari hilo kikafunguliwa. Magreth macho yakamtoka mara baada ya kumuona nabii Sanga. Bumbuwazi zito sana likamkamata Magreth na kujikuta akishindwa hata kumsalimia nabii Sanga.

“Huyu malaya ndio anaye tembea na mume wangu”

Mrs Sanga alizungumza kwa hasira hadi binti yake akashangaa.

“Malaya!!!”

Julieth alihamaki huku akitazama jinsi Magreth alivyo simama pembeni ya taksi hiyo.

“Ndio ana tembea na baba yake na hizi zote zilizo tumika hapa ni pesa za baba yako”

“Hapana bwana mama. Utakuwa una kosae, baba hawezi kuwa na mwanamke wa nje.”

“Mimi ndio ninaye mjua baba yako na si nyinyi na funga kinywa chako”

Mrs Sanga aliendelea kuzungumza kwa hasira kali sana.

“Suprize, najua umestuka sana kuniona hapa”

“U…u…me….e…fika…je hapa?”

Magreth alizungumza hukua akiwa amejawa na kigugumizi kizito sana.

“Nimeingia Tanzania kama lisaa moja lililo pita. Ingia ndani ya gari tuzungumze”

Magreth akashusha pumzi nyingi na kuzunguka upande wa pili wa gari hilo na kuingia ndani. Nabii Sanga akamuomba dereva kutoka ndani ya gari hilo kwani ana mazungumzo muhimu na bintu hiyo na dereva akatii jambo hilo.

“Unaona unaona dereva ametoka ndani ya gari na kuwaacha wao wawili”

“Tulia bwana mama, kwani dereva kutoka nje ya gari ndio kuna tatizo. Isitoshe lile eneo ni lawazi sana ambalo baba hawezi kujitokeza ikiwa ana waamini wengi sana. Mama hembu acha wivu wako”

Mrs Sanga akamtazama kwa hasira mwanaye huyo na kuachia msunyo mkali sana.

“Mbona umekuja bila kunitaarifu ikiwa uliniambia utarudi baada ya wiki?”

“Kwani kuna tatizo mpenzi wangu?”

“Hapana ila umenistua sana”

“Usijali, sogea hapa”

Nabii Sanga alizungumza huku akimsogeza kwa karibu Magreth, akaanza kumnyonya lispi zake.

“Jamani baby hapa kuna watu wengi na kumbuka nipo kazini.”

“Basi nina omba funguo nikakusubirie kwako. Leo sina hamu ya kwenda kulala nyumbani kwangu. Nimekumiss sana mpenzi wangu”

Mapigo ya Magreth yakazidi kumuenda kasi sana kwani nyumbani kwake amemuacha Evans ambaye ndio mwanaume anaye mpenda na hatamani hata siku moja kumpoteza.

“Aha….baby sasa kwa nini usiende nyumbani ukakutane na mama kwanza ina onekana atakuwa ame kumiss sana”

“Mama nimeachana naye uwanaja wa ndege. Nilikuwa naye kwenye ziara yangu yoye ya nchini Nigeria”

Kauli hiyo ikazidi kumuweka Magreth katika wakati mgumu.

“Nimekumiss sana Magreth wangu. Yaani kama kungekuwa hakuna wateja wengi hapa. Ningekuambia sasa hivi ufunge na tuondoke pamoja”

“Nime kumiss sana mume wangu. Ila nina kuomba uende nyumbani kesho sinto kuja kazini kwa ajili yako. Nitahitaji twende mbali na hapa Dar ess Salaam. Tukale raha sku nzima, kukaa nyumbani na ikiwa umetoka mbali mimi nina ona sio jambo zuri mume wangu. Ninataka tukakutane mbali, tupeane raha hadi nyeg** zituishe”

Magreth alizungumza kwa sauti ya upole na iliyo jaa mahaba mengi sana. Nabii Sanga akashusha pumzi huku akiuchukua mkono wa kulia wa Magreth na kuuweka juu ya jogoo wake.

“Mke wangu hembu tazama jinsi jogoo wangu alivyo simama. Ana hamuna wewe jamani”

“Hata mimi nina hamu naye jamani. Ila kesho nita mkatikia kama vile ninavyo mkatikia si utapenda nifanye hivyo. Leo nenda kapumzike, uzoee joto la Dar yetu hii ila kesho baba yangu kuanzia asubuhi ni mimi na wewe”

Nabii Sanga akatabasamu huku akitazama uzuri alio barikiwa Magreth.

“Kwa nini nisipende. Sawa mke wangu nimekuletea zawadi za garama sana. Kaa nazo hizi kesho kwenye hiyo safari zetu nina kuomba uwe nazo, nina hitaji nikuvishe mimi mwenyewe. Tafadhali usizifugue”

Nabii Sanga alizungumza huku akitoa mfuko wenye boksi lenye cheni hizo za garama pamoja na pete.

“Sawa mume wangu sinto zifungua”

“Nakuamini.”

Nabii Sanga akamvuta karibu Magreth na kuanza kumnyonya taratibu. Wakaachiana huku nabii Sanga akiwa amejawa na usongo mkubwa sana wa kupata penzi la Magreth.

“Acha niwahi nyumbani mke wangu kwa maana nikikaa hapa nita pandwa na mizuka bure”

“Hahaa sawa mume wangu. Nina kupenda sana”

“Ninakupenda pia. Ila vipi biashara ina kwendaje?”

“Ina kwenda vizuri sana”

“Mungu ni mwema, abariki katika hilo”

“Amen”

Magreth akashuka na mfuko huo wenye boksi dogo kisha taksi hiyo ikaondoka eneo hilo.

“Unaona ule mfuko ambao baba yako aliondoka nao pale uwanja wa ndege ndio amekuja kumuachia huyu malaya. Tuwahi nyumbani haki ya Mungu nina apa nita shuhulika naye mpumbavu. Hajui ni wapi nime toka na mume wangu alafu leo hii ana kuja kutumia pesa za mume wangu kirahisi namna hii”

Mrs Sang alizungumza huku machozi yakimlenga lenga usoni mwake. Julieth akamtazmaa kwa umakini Magreth na akaikremisha sura yake hiyo kisha wakaondoka eneo hilo huku wakijitahidi kupita njia ya mkato ili wawahi kufika nyumbani kabla ya nabii Sanga kufika.

Magreth akajikaza kutemeba hadi ndani ya mgahawa wake. Akatafuta kiti na kukaa huku akiwaza ni jinsi gani sasa ana weza kudili na nabii Sanga huku Evans akiwa nyumbani kwake.

“Ehee Mungu nisaidie nitafanya nini mimi?”

Magreth alijikuta akizungumza mwenyewe huku akiwa amejiinamia.

“Bosi kna tatizo?”

Juma alimuuliza Magreth huku akimtazama usoni mwake.

“Hapana hakuna tatizo”

“Nilisi labda yule bibi ame kutatiza tena”

“Hapana.”

Hamu ya kufanya kazi ikamuisha kabisa Magreth. Akasubiri hadi muda wa kufunga mgahawa wake, akapiga mahesabu ya kipato anacho kiingiza kwa siku hiyo na jambo la kumshukuru Mungu akajikuta akiwa ameingiza milioni kumi na mbili. Akampa kila mfanyakazi wake laki moja moja ikiwa kama bonus ya juhudi ya utendaji wao wa kazi. Magreth akawapa maagizo wahudumu wake hao, wahakikishe wana wahi kufika kazini asubuhi na mapema kwa maana na hati hati ya kuto kufika kazini siku inayo fwata. Mara baada ya maagizo hayo akaingia kwenye gari lake na kuelekea nyumbani kwake.

Akafika nyumbani kwake na Evans akamfungulia geti, akasimamisha gari lake kwenye maegesho na kumtazama Evans anaye funga geti hilo.

‘Ohoo Mungu wangu nita mueleza nini huyu mwanaume?’

Magreth aliwaza huku akishuka kwenye gari lake. Wakakumbatiana na Evans huku wakinyonyana ndimi zao. Wakaingia ndani kwa pamoja.

“Nimekuandalia chakula kizuri mke wangu. Nina imani hujakula huko kazini kwako?”

“Ni kweli mume wangu, acha nikajimwagie kwanza kisha nije tule kwa pamoja”

Wakaingia chumbani kwa pamoja.

***

Mrs Sanga na mwanaye wakawa wa kwanza kufika nyumbani hapo. Mrs Sanga hakuona hata haja ya kukaa sebleni hapo na kuzungumza na mwanaye huyo ambaye ni takribani mwenzi sasa hawajaonana. Baada ya lisaa moja nabii Sanga akafika nyumbani hapo na kupokelewa na Julieth pamoja na mfanyakazi wa ndani kwa furaha sana.

“Mama yenu yupo wapi?”

“Yupo chumbani”

“Vipi baba nikuandalie chakula?”

“Hapana, nitakula asubuhi. Ngoja nikampumzike”

Nabii Sanga akaondoka seblenii na kuingia chumbani kwake. Akamkuta mke wake akiwa amejilza kitandani, akavua nguo zote na kuingia bafuni. Mrs Sanga aliweza kusikia kila kitu mume wake anacho kifanya. Hakupata hata lepe la usingizi na kichwnai mwake ana panga mipango ya kuhakikisha ana mkomesha Magreth ambaye ana nufaika kwa pesa za familia yake.

“Mbona ume kaa au una usingizi?”

“Ulikwenda wapi?”

“Nilikwenda kukutana na mchangaji msaidizi wetu”

“Mchungaji msaidizi wetu!!!?”

“Ndio kwani kuna tatizo la mimi kuonana naye?”

“Hakuna sawa, nina hitaji haki yangu”

Mrs Sanga alimtega mume wake huku maana yake kubwa ya kumueleza hivyo ni kuona ni maamuzi gani ambayo ata yachukua.

“Nimechoka na safari nina omba nipumzike”

“Kwani hio safari ume safiri wewe mwenyewe na mimi pia si nilikuwa safarini?”

“Kwa hiyo, si kila mtu ana mwili wake wa kuchoka. Kwanza hembu kajisafishe hiyo najisi uliyo tiana na wanawake wezako kwa kusagana kisha ndio unifwate mimi nikupe haki yako”

“NAJISI!!?”

Mrs Sang aliuliza huku akiwa amejawa na hasira sana.

“Ndio mwili wako mzima hapo umejawa na najisi. Yaani binadamu mwenye akili zako timamu, una aamua kusagana na wanawake wezako una hisi kwamba wewe sio najisi. Yaani ni heri ya wanayama ambao hawana akili ila huwezi kuwaona wanyama wa jinsi moja wakifanya uchafu kama huo ulio ufanya wewe”

Nabii Sanga alizungumza kwa kejeli huku akimtazama mke wake aliye fura kwa hasira hapo kitandani.

“Ahaa..kwa hiyo hata wewe ni najisi kwa maana ulivyo kuwa una mfir** yule kijana wa watu ili utajirike na nikakusamehe na ukamfanya Tomas ulicho umfanya pia nika kusamehe. Leo hii una niona mimi nina nina makosa sana si ndio”

Mrs Sanga alizungumza kwa hasira huku akiwa amesimama mbele ya mume wake.

“Mimi nilikuwa nina fanya kwa sababu. Je wewe umenufaika na nini, zaidi ya kuchezewa chezewa, alafu leo hii una taka kuona mbo** yangu ina ingia kwenye kum** yako. Una akili kweli wewe, siwezi kuingia sehemu chafu kama hiyo”

Kauli za kejeli na dharau, zikamfanya mrs Sanga kupandwa na hasira sana na kujikuta akimzaba mume wake kofi zito la shavuni mwake huku akihema kwa hasira kali sana.

“Ole wako sikunyingine ufungue kinywa chako na kunitamkia upuuzi kama huo. Nipo radhi kukusambaratisha kwa kutoa siri zako zote na utajuta ni kwa nini uliwahi kuniona mimi na kunioa”

Mrs Sanga alizungumza kwa msisitizo huku akimyooshea nabii Sanga kidole cha usoni mwake akishiria kwamba alicho kizungumza ana kimaanisha na hatanii kwa jambo la aina yoyote ile.



“Hahaaaa……hahahahaaa”

Nabii Sanga alicheka sana kwa dharau huku akimtazama mke wake aliye fura kwa hasira. Nabii Sanga akajishika shavu lake alilo pigwa kibao. Akaushika mkono wa mke wake ambao ume mpiga kofi. Mrs Sanga akautoa mkono wake kwa nguvu huku akihisi kifua chake kina kwenda kumpasuka kwa hasira.

“Ngoja nikuambie jambo moja ambalo ulifahamu. Masharti ya utajiri wangu na huduma yangu yame badilika. Hayakutegemei wewe na wala huwezi kunisambaratisha. Kabla ya kufanya hivyo, wazazi wako na wadogo zako. Nitawapokonya kila kitu walicho nufaika kwa kupitia mimi. Wewe, nitakupokonya kia kitu unacho kimiliki kw amaana nilikuokota tu njiani kutoka mikononi mwa wale malaya wezako. Hivyo usi sahau kwamba kila mali na kila pesa unayo itumia ni vyangu. Kama una bisha acha nikuonyeshe jambo”

Nabii Sanga akatoa simu yake mfukoni huku akiwa amejawa na hasira. Akamuonyesha mke wake video ambayo ilirekodiwa pasipo kuja, yeye akifanya mapenzi na Tomas tena ofisini mwa mume wake. Japo alimuahidi mke wake kwangu alisha ifuta video hiyo ila bado anayo. Akamuonyesha video aliyo wafumania nyumbani kwa Tomas.

“Kwanza nina watumia wanao wote watatu. Washuhudie jinsi mama yako akiliwa jicho na kijana tena dalali. Kwanjia hiyo nitakuwa nime kupokonya upendo na support ya wanao. Nilazima watakuchukia na hakuna atakaye kuheshimu tena. Nitawapigia mameneja wote wa bank zenye akaunti yako, wata zifunga zote, sasa tuone kwama mimi na wewe nani mwenye nguvu na uwezo wa kumsambaratisha mwenzake”

Mrs Sanga akajikuta akinywea taratibu. Ni heri kufungiwa akaunti zake na asizitumie tena kuliko kutengenishwa na upendo wa wanaye ambao ana wapenda kupindukia.

“Sanga kwa nini ulinidanganya kwamba hizo video ume zifuta ingali bado zipo kwenye simu yako?”

“Naijua akili yako. Nikama kuku, ina shindwa kutambua mimi nime kutoa wapi n anime kuweka kwenye mazingira gani. Usijaribu wala kufikiria eti kuniangusha mimi. Hapana huto weza, japo tuna lala kitanda kimoja na kiishi nyumba moja moja ila bado huja nijua mimi. Nina roho ya kipekee sana ambayo ni wanadamu wachache sana ambao wana roho kama hiyo”

Nabii Sanga alizungumza kwa msisitizo huku akimtazama mke wake.

“Mume wangu ni hasira tu ila nina kuomba uni saheme”

“Kwani umenikosea?”

Mrs Sanga akabaki akiwa amejawa na kigugumizi. Nabii Sanga akamtazama kwa umakini mke wake, kisha akajifunga taulo na kutoka chumbani humo huku akiwa ameishika simu yake. Akamkuta mke wake na mfanyakazi wa ndani wakiwa wana tazama filamu sebleni.

“Baba bado huja lala?”

“Yaa bado. Ni filamu gani hiyo?”

“Ina itwa Jumanji”

“Ahaa ni nzuri ehee?”

“Yaa ina comedy ndani yake. Ehee baba vipi safari yako ime kwenda salama?”

“Ndio ime kwenda salama. Mikutano iliyo tupeleka huko ime kwisha salama”

“Ahaa Mungu ni mwema.”

Julieth akamtazama baba yake, akatamani sana kumuambia tukio walilo fanya na mama yake ila akajifariji kwamba ata mueleza mara baada ya kukutana na Magreth ili aweze kumuhoji. Nabii Sanga akaendelea kuzungumza mambo mengi na vijana wake hao. Hadi ilipo timu saa nane usiku, vijana wake wote waka ondoka na kuingia chumbani kulala. Nabii Sanga akaitafuta namba ya Magreth kwenye simu yake, akataka kumpigia ila moyo kidogo ukasita.

‘Ata kuwa amelala na amechoka kwa kazi yake ya mgahawa’

Nabii Sanga alizungumza kimoyo moyo na kuelekea chumbani kwake. Akamkuta mke wake akiwa amelala, taratibu na yeye akalala pembeni yake.

Julieth asubuhi na mapema akawahi kuamka. Akaoga na kujiandaa kwa ajili ya kuwahi chuo huku akilini mwake akidhamiria kuwahi kufika katika mgahawa wa Magreth kabla ya kwenda chuo. Kutokana alafajiri hiyo na mapema hakuna foleni kubwa. Akafanikiwa kufika katika mgahawa wa Magreth na kukuta wafanyakazi wawili.

“Bado hatujafungua ndugu Boss”

Mfanyakazi huyo wa kiume alimuambia Julieth huku akimatazama usoni mwake.

“Hakuna tabu, nita subiri hadi mufungue”

Julieth alizungumza huku akikaa kwenye moja ya kiti. Haukupita muda mrefu sana, Magreth akafika katika mgahawa wake, huku lengo la yeye kufika hapo ni kufungua tu ila siku hiyo mgahawa uta ongozwa na wahudumu wake kwani yeye ana safari ya kutoka nje ya jiji la Dar es Salaam. Magreth akamsalimia Julieth kama mteja tu, kisha akasalimiana na wafanyakazi wake na kuwakabidhi funguo.

“Samahani dada tuna weza kuzungumza?”

Julieth alizungumza huku akimfwata Magreth anaye minya minya simu yake akiitafuta namba ya nabii Sanga.

“Ndio tuna weza kuzungumza. Ila samahani mara moja”

“Sawa”

Magreth akaiweka simu yake sikoni huku akiendelea kusikilizia jinsi inavyo ita.

“Yes baby”

“Niambie mke wangu”

“Safi tu. Tuta kutana wapi?”

“Mmmm nina kuja hapa kwenye mgahawa wako au kuna watu wengi?”

“No tukutane nje ya hapa”

“Wapi tuonane?”

“Wewe kwa sasa upo wapi?”

“Mimi ndio nime ingia kwenye gari. Nina toka nyumbani”

“Basi wewe anza kutoka ila safari yetu ni nje ya Dar tuonane sehemua mbayo itakuwa ni rahisi kwa sisi kuendelea na safari yetu”

“Sawa mpenzi wangu. Basi ngoja kwanza nitoke alafu nitakuambia sehemu nilipo fika kisha nawe uta kuja”

“Poa, tutatumia gari langu au lako”

“Lako itapendeza zaidi”

“Sawa mume wangu nakupenda sana”

“Nakupenda pia”

Mazungumzo hayo ya Magreth, kidogo yakaanza kumuweka Julieth njia panda. Hisia za mama yake akaamini kwamba zimemfikiria vibaya dada wa watu, kwani ana mume wake anaye mpenda na ana zungumza naye kwa furaha namna hiyo.

“Ndio dada nina kusikiliza”

“Ahaa…..Samhani lakini kwa kukuuliza maswali yangu”

“Kuwa huru kabisa”

“Mimi nina itwa Anna”

Julieth alidangaya huku akimtazama Magreth usoni mwake.

“Nashukuru kukufahamu Anna. Mimi nina itwa Julieth”

“Nashukuru pia kukua jua. Ahaa……baba yangu alikuwa ana mpango wa kunifungulia mgahawa mkubwa sana. Ila nikashindwa kumpa jibu la moja kwa moja na nikamahidi nitakapo fanya research yangu kama hii biashara ina lipa basi ani fungulie kwa maana nina ogopa kufanya biashara ambayo kwa namna moja haito niigizia faida kama ile ninayo ihitaji”

Julieth alibadilisha mada japo alikwenda hapo kwa lengo moja tu, la kumuuliza maswali Magreth juu ya mahusiano yake na nabii Sanga.

“Ahaa hii biashara ni nzuri sana na ina faida kubwa sana. Chukua hii namba yangu ya simu kisha nipigie kama majira ya saa tatu usiku n ina imani kwamba nita kuwa nina muda mzuri sana wa kuzungumza na wewe”

“Sawa nashukuru sana”

Julieth akainakili namba aliyo tajiwa na Magreth kwenye simu yake kisha wakaagana na Julieth akaondoka pasipo kumgundua kwamba huyo aliye toka kuzungumza naye ni mtoto wa nabii Sanga. Magreth akampigia simu nabii Sanga na kumuomba waweze kukutana maeneo ya Mwenge na kwa bahati nzuri nabii Sanga amekaribia kufika maeneo hayo. Magreth akaingia ndani ya gari lake, ikamchukua nusu saa kufika katika eneo hilo. Nabii Sanga akaliacha gari lake katika moja ya sheli na kuliacha katika uangalizi wa sheli hiyo kisha akaingia kwenye gari la Magreth na wakainaza safari ya kuelekea nje kabisa ya jiji la Dar es Salaam.

“Hivi Bagamoyo kuta kuwa na usalama mpenzi wangu?”

Magreth alimuuliza nabii Sanga.

“Ndio kuna hoteli zipo ndani ndani sana na ninzuri sio rahisi kwa mtu kuweza kufahamu kwamba tupo pale.”

“Hapo sawa kwa maana si una tambua wewe mwenzangu ni maarufu. Isije mashilawadu wakaanza kutupiga picha na kuzisambaza kwenye mitandoa ya kijamii nina imani kwamba mke wako ata tuua”

“Hahaa usiogopea”

Nabii Sanga alizungumza huku akilitomasa tomasa paja la Magreth lililo nona vizuri na kutamanisha.

***

Julieth kila anavyo jaribu kujishauri kuelekea chuoni, moyo wake una sita kabisa na kujikuta akianza safari ya kuelekea nyumbani kwao. Akamkuta mama yake akiwa sebleni ame kaa kiunyonge sana.

“Vipi mbona ume rudi, huja kwenda chuo?”

“Ndio mama, shikamoo”

“Marahaba. Ehee kwa nini huja kwenda chuo”

“Baba yupo?”

“Hapana ame ondoka alfajiri na mapema”

“Amesema ana kwenda wapi?”

“Haja nieleza chochote”

“Hajakuaga?”

“Ndio. Mbona una uliza sana?”

Julieth akamsogelea mama yake sehemu alipo kaa.

“Nimetoka kwenye ule mgahawa tulio kwenda jana na nime kutana na yule dada”

Mrs Sanga akaka vizuri kwenye sofa hilo, kwani huyo anaye zungumziwa hapo ni mwizi wake.

“Ulikwenda kufanya nini?”

“Nilikwenda kujidhibitishia kwamba je ana mahusiano na baba au laa. Ila kwabahati nzuri mume wake alipiga simu pale na akazungumza naye vizuri sana. Ikabidhi nibadilishe mada na kumueleza kwamba na mimi baba yanu amepanga anifungulie mgahawa.”

“Hakuweza kukufahamu kwamba wewe ni mtoto wa nabii Sanga?”

“Ndio hakunifahamu na jina nilimueleza kwamba nina itwa Anna na akaniachia namba yake ya simu”

“Unayo hapo?”

“Ndio ninayo”

“Nionyeshe hapo”

Julieth akamuonyesha mama yake namba hiyo ya simu. Akainakili kwenye simu yake na akata kumpigia Magreth ila akasita kidogo.

“Mama usimpigie, taratibu twende naye huyu ili tujue ni kitu gani kinacho endelea. Nimeamua kukusaidia mama yangu kwa sababu nina kupenda na sipendi kukuona ukiwa katika hali mbaya ya kufedheheka kisa baba”

Julieth alizungumza kwa suati ya upole na iliyo jaa faraja sana. Taraibu Mrs Sanga akamkumbatia mwanaye huyo wa mwisho.

“Nime pata wazo”

“Wazo gani?”

“Kuna dada mmoja hivi nina mfahamu ana dili na maswala ya IT. Pia ana kampuni ya mambo hayo. Anaitwa Levina ni rafiki yangu japo sio sana. Anaweza kunisaidia katika kui hack namba ya huyo dada ili tuweze kusikia kila anacho kizungumza katika simu yake.”

Julieth alizungumza wazo ambalo mama yake hakuweza kulipinga kabisa. Julieth akampigia simu Levina na wakapanga kukutana ofisini kwake asubuhi hiyo. Mrs Sanga akajiandaa haraka haraka na wakaifunga safari na binti yake kuelekea ofisini kwa Levina. Wakafika ofisini hapo na kuruhusiwa kuingia ndani, Levina akastuka kidogo kumuona mrs Sanga hapo, kwani alisimuliwa na Tomas kwamba mwana mama huyo alielezwa sira juu ya mchepuko wa mume wake na mume wake aliamua kumsingizia Tomas kesi iliyo mfanya atafutwe na askari nchi nzima, japo hata story hiyo aliyo elezwa na Tomas haina ukweli. Ila ukweli ni kwamba huyo ni mke mwezie.

“Karibun sana”

“Tunashukuru Levina. Bwana nimekuja na shida moja hapa nina kuomba uweze kutusaidia”

“Hakuna tatizo ni nyinyi tu”

“Huyu ni mama yangu mzazi.”

“Nashukuru sana kukufahamu mama”

“Asante”

“Ngoja nikueleze jambo lililo tuleta hapa. Kuna msichana mmoja hapa mjini mama ana hisi kwamba ana mahusiano na baba. Msichana huyo inavyo sadikika ame funguliwa mgahaw ana baba. Sasa kitu ambacho nina hitaji ukifanye ni kuhack simu yake, ili simu zote zinazo ingia kwenye simu yake sisi nasi tuweze kusikia”

“Mmmm hiyo kazi ni rahisi sana. Ila watu wengi ambao nime wafanyia hiyo kazi. Wengi wameishia katika kuwadhuru wapenzi wao na wengine ndoa zao kuvunjika. Sinto pendelea kuona kwamba nina isambaratisha ndoa ya mtumishi wa bwana mkubwa kama nabii Sanga kwa ajili ya kazi yangu”

Levina alizungumza kwani jambo hilo sio mara yake ya kwanza kulisikia, ni mara ya pili kwa nabii Sanga kuhusishwa na msichana huyo na kesi ikiwa ni hiyo hiyo ya msichana huyo kufunguliwa mgahawa.

“Nisikilize binti yangu. Sisi hapa wote ni wanawake, tuna mioyo ya kuumia, wewe mume wako akikuumiza ni lazima uta umia. Nina kuomba unisaidie kama mama yako, nahitaji mazungumzo yanayo ingia kwenye simu ya biti huyo tu na wala sihitaji mazungumzo yanayo ingia kwenye simu ya mume wangu”

Mrs Sanga alizungumza kwa sauti ya upole sana na iliyo jaa unyenyekevu. Levina akamtazama mrs Sang.

‘Nitamsaidia Tomas katika kuanza kulipiza kisasi chake’

Levina alizungumza kimoyo moyo. Wakakubaliana kiasi cha shilingi milioni tano na Levina akaianza kuifanya kazi hiyo. Ndani ya dakika tano akafanikiwa kuhack mazungumzo yote yanayo ingia kwenye simu ya Magreth yawe yana ingia pia katika simu ya mrs Sanga pamoja na Julieth.

“Kazi yenu ime kwisha”

“Tuna shukuru sana Levina. Ila kuna simu moja alipigiwa asubuhi hii ya leo. Je mazungumzo yake tuna weza kuyapata?”

Julieth alizungumza huku akimtazama Levina usoni mwake.

“Ndio yapo hapa”

“Je tuna weza kuyasikia?”

“Muna hakika muna hitaji kuyasikia?”

“Ndio”

Levina akawatazama Julieth na mama yake, kutokana wame amaua kusikia mazungumzo yaliyo pita katika simu ya Magreth akaminya batani katika laptop yake na mazungumzo kati ya Magreth na nabii Sanga yakaanza kupenya taratibu masikioni mwao na kumfanya Julieth kushangaa sana huku mama yake akiwa ame fura kwa hasira kali sana ya kuibiwa mume wake na Magreth.



“Wa…a…me…sema wana kwenda Bagamoyo?”

Mrs Sanga alizungumza huku akibabaika sana. Hakuweza hata kukaa kwenye kiti hicho, akanyanyuka na kuanza kuzunguka zunguka ndani ya chumba hicho huku mapigo yake ya moyo yakimuenda kasi.

“Mama tulia basi, kufanya hivyo maana yake nini?”

Julieth alizungumza kwa msisitizo huku akimtazama mama yake usoni. Levina akatabasamu huku akimtazama mwana mama huyo kwani sasa ana zidi kumchanganya mwanamke huyo.

“Binti hembu jaribu kuitafuta namba ya mume wangu nataka kujua kwa sasa yupo wapi?”

“Hiyo ni kazi nyingine mama. Je uta nilipa?”

“Pesa sio shida. Wewe fanya kama nilivyo kueleza”

Levina akaitafuta namba ya nabii Sanga, haikuchukua muda sana akafanikiwa kufahamu ni sehemu gani nabii Sanga yupo.

“Mume wako yupo Bagamoyo kwa sasa”

“Na huyo malaya si yupo huko huko Bagamoyo?”

“Wapo eneo moja”

“Niamabie ni eneo gani wapo nahitaji kwenda sasa hivi”

Mrs Sanga alizungumza huku jasho likimwagika usoni mwake. Levina akachukua kikaratasi kidogo na kuandika jina la eneo walipo nabii Sanga na Magreth, pamoja na hoteli, kisha akamkabishi mrs Sanga kikaratasi hicho.

“Malipo yangu”

“Ni kiasi gani?”

“Hi kazi ya sasa niliyo kufanyia ni milioni mbili”

Mrs Sanga akahamisha kiasi cha milioni saba kwenye akauti ya Levina kisha akwaondoka eneo hilo huku mrs Sanga akitamani hata apae angani ili kufika eneo la Bagamoyo.

“Naomba funguo zako”

“Mama siwezi kukufa funguo ya gari ukaendesha. Acha niendeshe mimi mwenyewe”

“Usiniletee ujinga. Nipe funguo ya gari”

Mrs Sanga alimfokea sana Julieth ambaye hakuwa na jinsi zaidi ya kutii amri hiyo ya mama yake. Akamkabidhi funguo ya gari lake kisha wakaingia. Mrs Sanga akalirudisha nyuma gari hilo kwa kasi kisha akaliweka sawa. Safari ya kueleke Bagamoyo ikaanza huku akiwa katika mwendo wa kasi sana.

“Mama taa inashawaka ya orange punguza mwendo”

Julieth alimuambia mama yake, huku akizitazama taa za barabarani eneo hilo la Mwange. Hadi anakaribia kufika eneo la makutano ya taa hizo, tayari taa nyekundu ilisha waka kwa ishara ya kuwaashiria kwamba wasimame, na taa za upande wa kulia zikaruhusiwa. Mrs Sanga hakujali kuwashwa kwa taa hizo nyekundu na kujikuta akijitahidi kukatiza, ila gafla bodaboda aliye mpakiza abiria, tayari walishajaa mbele ya gari lao na kujikuta akiwabamiza kwa nguvu huku akifunga breki za gari hilo na kuzifanya tairi za gari hilo kuserereka kwa muda kisha gari likasimama huku mrs Sanga akiwa amejawa na hofu kubwa sana na tayari waendesha pikipiki wa eneo hilo pamoja na watu wengine wameanza kulisogelea gari hilo huku wakionekana kujawa na hasira kali sana.

***

Mara baada ya kupata kifungua kinywa, Evans akajiandaa kwa safari ya kwenda kuonana na mmoja wa wanachuo alio maliza nao kusoma. Evans akaichu simu yake inayo ita, akaipokea na kuiweka sikioni mwake.

“Niambie kaka”

“Vipi bado hujatoka?”

“Nipo njiani ndugu yangu ninakuomba unisubirie”

“Wahi ndugu yangu si unajua kwamba kuna ratiba nina hitaji kuiwahi mida ya saa sita hivi”

“Poa poa kaka”

Evans akakata simu na kumaliza kujianda, akachukua kiasi cha pesa na kuweka katika katika wallet yake. Kutokana Magreth ameondoka na gari lake, ikamlazimu Evans kukodisha pikipiki.

“Hadi Masaki ita garimu kiasi gani?”

“Hapo itakuwa ni elfu arobaini”

“Sawa nina omba helment”

“Lipo hili hili moja kaka”

“Sawa nina liomba nivae mimi. Ila si munapaswa madereva bodaboda si munatakiwa kuwa na helment mbili?”

“Ndio kaka ila vaa hili, tukifika hapo mbele nitawaomba jamaa maskani”

Muendesha pikipiki huyo akamkabidhi Evans kofia hiyo ngumu ya kujilinda kichwa pale kinapo pata tatizo kama ajali. Safari ikaanza kuelekea masaki, ila walipo kuwa njiani Evans akamuomba dereva huyo wapitie Mlimani City kuna jambo ambalo ana hitaji kulinunua.

Wakafanikiwa kufika Mlimani City na Evans akaingia ndani ya jengo hilo lenye maduka mengi. Akafika katika duka linalo uza bidhaa za kampuni ya apple. Akaulizia bei ya moja ya laptop.

“Basi nitakuja kuichukua by saa saba”

“Sawa kaka karibu sana”

Evans akatoka dukani hapo na kurudi alipo muacha muendesha pikikipi.

“Kaka kiasi kitaongezeka kidogo”

“Sawa hakuna shaka”

Wakaondoka eneo hilo, wakafika Mwenge na kusimama kwani taa za upande wao zimewazuia. Baada ya dakika moja taa za upande huo zikawaka. Dereva wa pikipiki akatia gia na kuondoka, kitendo cha kufika katikati ya eneo hili la makutano ya mataa hayo, gari moja ikawagonga, Evans akarushwa pembeni na kuanza kubingirika kwenye lami hiyo huku muendesha pikipiki akirushwa na pikipiki yake huku akivunjika vujika kwani yeye ndio amebamizwa vibaya sana na pikipiki hiyo. Evans akasimama huku akishangaa jinsi watu wanavyo zidi kujaa katika eneo hilo. Akatazama jinsi watu wanavyo mfwata muendesha pikipiku aliye laliwa na pikipiki yake huku hali yake ikizidi kuwa mbaya.

“Upo salama wewe?”

Jamaa mmoja alimuuliza Evans ambaye bado hajielewi. Kila anacho kiona katika eneo hilo ana ona kama ni filamu fulani.

“Mkalishe chini huyo hapo sio yeye”

Jamaa mmoja alizungumza, wakamshika Evans mkono na kumtoa katikati ya barabara hiyo na kumkalisha pembeni huku wakijaribu kumtazama kama ana majera ya aina yoyote.

“Oya una nijisiaje?”

“Nipo poa”

“Kweli?”

“Ndio nipo sawa”

Evans akatoa simu yake mfukoni na kuitazama, akakuta kioo kikiwa kimepasuka kwa kuvunjika vunjika vibaya. Raia wenye hasira kali wakaendelea kuwalazimisha watu walio wagonga Evans na muendesha pikipiki huyo kushuka ndani ya gari huku wengine wakitishia kuvunja vioo vya gari hilo. Askari wa jeshi la kutuliza ghasia ambao walikuwa katika eneo la sheli katika makutano hayo, wakafika eneo la tukio na kuanza kuzungujmza na wananchi hao wenye hasira. Ila wananchi hao wakaonekana kuto kukubaliana na mazungumzo hayo ya askari. Askari mmoja akakoki bunduki yake aina ya SMG na kupiga risasi mbili hewani na wananchi hao wakaanza kutawanyika huku kila moja akiogopa milio hiyo. Askari hao wapatao nane, wakalizunguka gari hilo na askari mmoja akamuamrisha mwana mama anye endesha gari hilo kufungua.

Mrs Sanga wala hakuwa na nguvu ya kufungua mlango wa gari hilo. Julieth muda wote huo wameshikwa na bumbuwazi kiasi kwamba haelewi kinacho endelea.

“Mama fungua mlango”

Askari huyo alizungumza huku akipiga piga kioo cha gari hilo. Mrs Sanga akamtazama askari huyo, akashusha pumzi, kisha akaminya batani na kufungua lock za mlango huo.

“Mama shuka”

Askari huyo alizungumza kwa ukali sana. Mrs Sanga machozi yakaendelea kumwagika usoni mwake pasipo kuzungumza kitu chochote. Askari huyo akafungua mkanda wa siti wa mrs Sanga na kumshusha ndani ya gari hilo.

“Mpelekeni kule”

“Askari mmoja alizungumza huku akiwa amemshika kisawa sawa mrs Sanga. Baadhi ya watu walipo katika eneo hilo waliweza kumfahamu mrs Sanga. Mrs Sanga akapakizwa kwenye gari hilo la askari, huku askari mwengine akiingia kwenye gari la Mrs Sanga, wakampakiza Evans, huku dereva pikipiki akipakizwa kwenye gari jengine la msamaria mwema kuwahiswa hospitali. Askari huyo akafika hospitali ya Lugalo.

“Jamani hapa ni wapi?”

Julieth alistuka kutoka katika hali ya kuduwaa.

“Lugalo hapa”

Askari huyo alimjibu Julieth ambaye bado ana endelea kushangaa shangaa.

“Oya dogo shuka. Wewe demu, hii gari ipo chini ya ulinzi, kama ina wezekana shuka hapa nina ipeleka kituoni central”

“Kwani kuna nini kimetokea na mama yangu yupo wapi?”

“Kwani hukumuona mama yako ame gonga watu. Huyo jamaa ni mmoja wa watu walio gongwa. Oya dogo shuka kabisa”

Evans akafungua mlango wa gari hilo na kushuka. Wakaongozana na askari huyo hadi mapokezi, wakafungua jalada la matibabu na akamkabidhi Evans kwa daktari huyo kwa ajili ya matibabu.

“Samahani afande ahaa....mama yangu amepelekwa wapi?”

“Central polisi”

“Naweza kuongozana na wewe?”

“Itakulazimu kukaa na mgonjwa hapa na matibabu yote atakuwa juu yenu. Baada ya hapo njooni central polisi”

“Sawa samahani, ninaomba nichukue vitu vyangu ndani ya gari”

“Fanya haraka”

Julieth akachukua pochi yake pamoja na simu ya mama yake, kisha askari huyo akaingia ndani ya gari na kuondoka eneo hilo. Julieth akaitafuta namba ya baba yake na kumpigia simu.

***

Nabii Sanga, akamsukumia Magreth kitandani huku akiwa amejawa na usongo wa kuhakikisha kwamba ana ikata kiu yake ya mahaba kwa Magreth. Akaanza kuvua shati taratibu huku akimtazama Magreth aliye zidi kunona. Mlio wa simu ukamfanya nabii Sanga kuanchia msunyo mkali sana, kwani toka waingie hotelini hapo amesahau kuizima simu yake. Akaitoa mfukoni na kutaka kuizima, ila alipo ona jina la binti yake akashusha pumzi kidogo na kuipokea simu hiyo.

“Baba kuna matatizo makubwa sana”

Kauali hiyo ya Julieth aliyo itoa pasipo hata salamu, ikamstua sana nabii Sanga.

“Matatizo gani?”

“Yaani hapa ninapo kuambia mama ameshikiliwa na polisi na amepelekwa central polisi.”

“Ameshikiliwa na polisi!! Amefanya kosa gani?”

Kauli hiyo ikamfanya Magreth kukaa kitandani huku akimtazama nabii Sanga ambaye tayari ana onekana kama kuchanganyikiwa.

“Amegonga muendesha pikipiki pamoja na abiria wake”

“Ohoo Mungu wangu. Hao alio wagonga wapo hai au wamekufa?”

“Mmoja nipo naye hapa Lugalo, ila huyu kidogo hali yake inaridhisha. Ila huyo muendesha pikipiki sijamuona kabisa”

“Umesema mama yako amepelekwa kituo gani?”

“Central”

“Nina kuja hapo Lugalo sasa hivi”

“Sawa baba, ila kamtoe mama”

“Sawa, ila acha nije hapo”

Nabii Sanga akakata simu na kuirudisha simu yake mfukoni. Akaanza kufunga vifungo vya shati lake.

“Mume wangu kuna kitu gani kinacho enelea?”

“Mke wangu ame gonga muendesha pikipiki pamoja na abiria wake”

“Ohoo Mungu, sasa ina kuwaje?”

“Tuondoke tu, kwa leo imeshindikana mke wangu. Ule mfuko wa zawadi nilio kupa upo wapi?”

“Nimeuwacha ndani ya gari”

“Twende”

Nabii Sanga na Magreth wakachukua kila walicho ingia nacho. Wakaingia ndani ya gari hilo, nabii Sanga akafungu mfuko huo na kutoa boksi la cheni hizo zenye thamani kubwa sana ya pesa.

“Waooo baby asante sana”

“Usijali mke wangu ni zawadi ndogo tu hiyo. Utaendelea kupata vitu vingi sana ukiwa na mimi”

“Nashukuru sana”

Wakaondoka eneo hilo huku nabi Sanga akianza kutafuta namba ya RPC Karata, akampigia na simu ikapokelewa.

“Naona umenitafuta mara baada ya matatizo yangu kuisha si ndio?”

Kauli ya RPC Karata kidogo ikampa kigugumiza nabii Sanga cha kuzungumza jambo ambalo anahitaji kumueleza kiongozi huyo wa jeshi la polisi kwa mkoa huu wa Dar es Salaam.

“Samahani ndugu yangu. Nina jambo moja ambalo ndio limenifanya nikupigie. Nimesikia mke wangu ameletwa hapo kituoni kwako. Ningependa kujua ni utaratibu gani una fwata?”

“Utaratibu ulipo hapa ni kwamba mke wako atapelekwa moja kwa moja Segerea na katika hili mzee wangu, tafadhali usinihusishe kabisa katika jambi hili kwa maana sinto kusaidia chochote na habari mbaya iliyopo sasa hivi. Yule bodaboda aliye gongwa na mke wako ame fariki dunia hivyo jiandae kifikra mke wako ana shikiliwa pia kwa kosa la mauaji. Nakutakia siku njema”

RPC Karata akakata simu na kumfanya nabii Sanga kuanza kujawa na wasiwasi mwingi sana huku mapigo yake ya moyo yakianza kumuenda kasi sana.



“Vipi?”

“Bodaboda aliye gogwa na mke wangu amefariki hivyo mke wangu ana shitakiwa kwa kosa la mauaji”

“Mmmm sasa itakuwaje mpenzi?”

“Yaani kichwa changu hapa kimechanganyikiwa”

“Ila kabla ya kuondoka si ulikwenda kuonana na raisi ikulu. Jaribu kuwasiliana naye”

“Alafu kweli nashukuru kwa kunikumbusha nakupenda sana”

Nabii Sanga alizungumza huku akiitafuta namba ya simu ya raisi Mtenzi. Akaipata na kumpigiam kwa bahati mbaya akakuta namba ya raisi ikiwa haipatikani.

“Muheshimiwa hapatikani”

“Jaribu labda ina weza kuwa ni mtatando”

Nabii Sanga akajaribu tena kumpigia raisi ila hakuweza kumpata kabisa. Wakafika maeneo ya Lugalo na Magreth akasima gari pembezoni mwa barabaka kama jinsi nabii Sanga alivyo mueleza aweze kufanya hivyo.

“Ngoja nishuke hapa. Mimi nina ingia kwanza huku hospitalini. Wewe nenda kwenye mgahawa tuta wasiliana mara nitakapo tatua tatizo hili”

“Sawa mpenzi wangu”

Nabii Sanga akamnyonya Magreth denda kidogo kisha akashuka katuka gari hilo. Magreth akaondoka na kurudi kwenye mgahawa wake. Nabii Sanga akaingia hospitalini hapo na kuwasiliana na Julieth, akamuelekea sehemu alipo na wakakutana.

“Vipi hali ya mgonjwa?”

“Bado hajatolewa chumba cha matibabu”

“Aliye pata ajali ni mwanaume au mwanamke?”

“Ni mwanaume”

“Sasa wewe baki hapa. Ngoja nielekee polisi nikaangalie ustarabu wa mama yako”

“Haya”

“Pesa ya kulipa matibabu si unayo”

“Labda uniongezee incase kumetokea tatizo lolote basi niweze kulirekebisha”

NabiI Sanga akatoa kiasi cha shilingi laki tatu na kumkabidhi Magreth. Watu wengi katika eneo hilo, hawakusita kumkodolea macho nabii Sanga. Nabii Sanga akatoka nje ya hospitali hiyo, akakodisha bajaji na kuondoka. Evans akatoka katika chumba cha matibabu huku akiwa amefungwa fungwa bandeji kwani baadhi ya meeneo katika mikono yake ime chubuka. Magreth akamfwata Evans sehemu alipo simama na kuanza kujing’ata ng’ata.

“Aaha…naitwa Julieth”

“Nashukuru kujujua”

“Mama yangu ndio aliye wasababishia ajali. Samahani kwa hanvi hilo”

“Usijali jambo kubwa ni kumshukuru Mungu nimekuwa salama na sijapata madhara yoyote ya ndani zaidi ya hii michubuko”

“Sawa. Nimepewa jukumu la kulipia matibabu yako yote.”

“Usijali nitalipia”

“Hapana ni jukumu letu kufanya hivyo kwa maana sisi tume wasababishia matatizo makubwa sana. Hivyo nina kuomba niweze kulifanya hili kazi”

Evans akakubaliana na alilo ambiwa na Julieth. Baada ya Julieth kufanya malipo, wakaruhusiwa kuondoka hospitalini hapo.

“Una itwa nani kaka?”

“Evans”

“Mimi nina itwa Julieth”

“Nashukuru kukufahamu.”

“Naweza kupata namba yako ya simu?”

“Ndio, japo simu yangu kwa sasa ime pasuka kioo ila una weza kupata”

Evans alizugumza huku akiitoa simu yake mfukoni. Julieth akaitazama kwa muda kidogo kisha akatingisha kichwa akioenekana kujawa na masikitiko makubwa sana. Julieth akaitazama saa yake ya mkononi na kukuta ni saa sita na dakika tano.

“Tunaweza kuelekea Mlimani City nika kununulie simu kama hiyo?”

“Usijali dada yangu. Acha tu ni mambo madogo sana”

“Hapana Evans, natambua fika haukuwa na mpango wa kununua simu mpya tena ya garama kama hiyo iphone X. Tafadhali nina kuomba nikafanye hivyo”

Evans akashusha pumzi taratibu huku akimtazama Julieth ambate ni binti mzuri sana na anavyo onekana ni msichana wa matawi ya juu.

“Sawa”

Wakakodisha bajiaji na wakainza safari ya kuelekea Mlimani City.

***

Mrs Sanga akaingizwa kwenye mahabusu ya kwake peke yake, hii yote ni kutoakana na heshima na kujulikana kwa mume wake. Muda wote mrs Sanga yupo kwenye hali ya kulia kwa uchungu sana. Ana tamani sana jambo hili liwe kama ndoto kwenye maisha yake. Akakumbuka jinsi mwanaye alivyo msisitizia kupunguza mwendo ila kutokana na hasira zake zilizo changanyikana na wivu, alijikuta akivunja sheria za barabara na kugonga watu hao.

Nabii Sanga mara baada ya kuchukua gari lake alilo kuwa ameliacha maeneo ya mwenge. Akafika kituoni hapo, akaomba kuzungumza na RPC na akaaombwa kuweza kumsubiria kwa maana RPC ana kikao.

“Je mke wangu nina weza kumuona?”

“Ndio nabii”

Nabii Sanga akapelekwa katika mahabusu aliyo wekwa mke wake. Mrs Sanga akanyanyuka kwa haraka mara baada ya kumuona mume wake akiwa amefika eneo hili.

“Ohoo asante Mungu kwa kuja mume wangu”

“Niambie ni nini kilicho tokea?”

Nabii Sanga alimuuliza mke wake ambaye mashavu yake yamelowana kwa machozi.

“Ni…nii….megonga mume wangu”

“Ilikuwaje kuwaje mke wangu hadi ukafanya jamb kama hilo?”

“Sijui mume wangu, ilitokea tu”

“Ahaa unajua yule uliye mgonga ame……..”

Nabii Sanga alijikuta akikatisha sentensi yake huku akimtazama mke wake, anaye tia huruma. Jeuri na ujanja wote ume muishia.

“Mume wangu fanya unitoea”

“Ndio maana nipo hapa. Acha nifanye michakato kisha nitakujulisha ni wapi ambapo nimefikia.”

“Sawa, ila mume wangu nina kutegemea mimi nakuomba usiniache nikae humu”

“Usijali mama Julieth, nita hakikisha kwamba leo hii hii una toka”

“Samahani mchangaji. RPC ana kuhitaji ofisini kwake”

Askari mmoja alimuambi nabii Sanga. Wakaongozana na askari hyo hadi ofisini kwa RPC Karata.

“Karibu uketi”

Nabii Sanga akaka kwenye kiti hicho huku akimtazama kijana huyo.

“Naomba kujua hili jambo lina uzito gani na nini nifanye ili niweze kumto mke wangu?”

“Sina cha kukusaidia. Andaa mwana sheria wako kwa ajili ya kwenda kusimama mahakamani na mke wako hawezi kupata dhamana”

RPC Karata alizungungumza kwa kujiamini kwani mzee huyu alimfanya aingia kwenye matatizo ambayo chupuchupu angepoteza ajira yake na kupotelea jela.

“Karata nakuelewa ni kwa nini una kuwa hivyo kwangu. Ila kwa jambo lile lililo jitokeza nyuma nina omba unisamehe”

“Hivi kama mke wako asinge pata matatizo kama haya. Unge niomba masamaha kweli? Jibu ni hapana kwa maana ni takribani mwenzi mmoja una kwenda wa pili sasa. Upo kimya sana wala hujathubutu hata kunitumia meseji. Ila ngoja nikuambie kitu kimoja mzee wangu, kipindi cha nyuma nilikuwa nina kuheshimu sana, tena sana. Ila mara baada ya kutambua upuuzi wako unao ufanya, yaani nina mashaka kabisa na hiyo huduma yako ya kuwaongoza hao unao waita ni kondoo wa bwana.”

“Karata huko unapo kwenda ni mbali sana. Hupaswi kuzungumza hivyo kumbuka wewe ni muumini wangu mzuri sana wa kanisani kwangu”

“Nilikuwa muumini wako, ila kwa sasa huto ona pua yangu wala familia yangu ikija kanisani kwako.”

“Sawa nina shukuru, ila roho wa bwana akakusimamie wewe na familia yako”

“Yaani huyo roho aanze kukusimamia wewe na familia yako. Mimi simtaki kabisa, naona muda wako ume kwisha una weza kwenda na nimewaambia hao vijana wangu kwamba. Mkewako hapaswi kupewa dhamana”

RPC Karata alizidi kuzungumza kwa kujiamini sana na kumfanya nabii Sanga kuzidi kujawa na hofu, kwani mke wake kuendelea kuwemo ndani ya mahabusu hizo ni aibu kubwa sana. Simu ya nabii Sanga ikaanza kuita, akaitoa mfukoni, moyo wake uka lipuka kwa furaha mara baada ya kuiona namba ya raisi ikimpigia. Akaipokea simu hiyo na kuweka sikioni.

“Habari za masiku muheshimiwa?”

“Salama kabisa nabii Sanga. Nimekuta meseji, zinaonyesha kwamba uli nitafuta”

“Ni kweli muheshimiwa raisi. Nina tatizo mheshimiwa”

RPC Karata akaka vizuri kwenye kiti chake mara baada ya kusikia nabii Sanga akizungumza na raisi.

“Tatizo gani mtumishi?”

“Leo mke wangu aligonga vijana wawili. Kwamujibu wa RPC hapa ameniambia kwamba kijana ambaye aliendesha pikipiki amefariki dunia na hivi sasa mke wangu bado yupo mahabusu. Nilikuwa nina kuomba muheshimiwa kama ikiwezekana aweze kupewa dhamana”

“Sawa nabii nimekusikia. Ila unatambua kwamba hilo ni kosa la mauaji, kama aliwagongwa kwa bahati mbaya basi kesi ina weza kuwa rahisi kidogo mahakamani. Ila kama alimgonga makusudi kesi ita kuwa ni ngumu”

“Ni kweli muheshimiwa, ila nina omba unisaidie japo apate dhamana”

“Mmmm kwa kweli nabii Sanga, labda nikuombe samahani. Hilo jambo mimi sinto weza kulifanya kwa maana utawala wangu una endeshwa kwa haki sawa. Kujuana kwetu basi kusiwe ni sababu ya kusaidiana kwa matatizo kama hayo. Endapo nitakusaidia leo, hakika nitakuwa nime kwenda kinyume na kiapo changu. Ngoja tuangalie sheria ita fanya nini”

Nabii Sanga akahisi nguvu zikimuishia kwani mtu ambaye alikuwa amemtegemea ndio hiyo ame mkatili kwa kukataa kabisa kuweza kumsaidia.

“Sawa muheshimiwa raisi nashukuru sana kwa ushauri wako mzuri”

Nabii Sanga alizungumza kwa sauti ya huruma ila moyoni mwake dhairi moyo wake umechukizwa na majibu hayo ya muheshimiwa raisi.

“Sawa karibu sana ikulu”

“Nitakaribia”

Simu ikakatwa. RPC Macho yakamtoka huku akisubiria kauli yoyote ya nabii Sanga. Simu ya mezani ya RPC Karata ikaanza kuita, akaipokea.

“Karata huyo Sanga yupo ofisini kwako?”

“Ndio muheshimiwa”

“Basi hembu mpeni dhamana mke wake. Ila kesi iwepo pale pale”

“Sawa muheshimiwa”

“Ila hakikisheni familia ya huyo kijana ina pata stahiki zinazo paswa kuweza kupata”

“Nimekuelewa mueshimiwa”

“Haya”

RPC Karaka akakata simu huku akimtazama nabii Sanga usoni mwake.

“Naona sasa una kula na wakubwa”

RPC Karata alizungumza huku akiwa amejawa na hasira kali sana. Maamuzi yake ilikuwa ni kuhakikisha kwamba mrs Sanga ana pata maumivu kama wanayo yapata watu wenye maisha ya chini.

“Kama wewe ulishindwa kunisikiliza, basi mimi nina panda juu zaidi. Ili tuone ita kuwaje”

“Ahaa…kwa hiyo ume kuwa mjanja sasa?”

“Mimi ni zaidi ya mjanja ndio maana nina pesa nyingi hata za kulinunua hili jeshi la polisi lote na kulilipa mishahara na madeni yote wanayo idai serikali na pia pesa zangu zita bakia”

“Mzee Chunga mdomo wako. Heshimu jeshi langu, hii kazi si ya kukurupuka”

RPC Karata alizungumza kwa ukali huku macho akimkodolea nabii Sanga.

“Acha kunikodolea macho kama mjusi aliye banwa na mlango.”

Nabii Sanga alizungumza huku akicheka kicheko kilicho jaa dharau kubwa sana. RPC Karata akanyanyua mkonga wa simu yake na akaagiza mrs Sanga aletwe ofisini kwake.

“Mzee usijidanganye kwamba ume shinda. Siku zako zina hesabika na endapo utaingia kwenye kumi na nane zangu. Haki ya Mungu nina kupoteza”

“Hahahaaa……wewe Karata ndio wa kunitisha mimi. Hapana kwa kweli, ngoja nikuambie ukweli. Nina mamlaka ya kukufanya wewe uhame mkoa huu na kwenda mkoa mwengine ndani ya siku yoyote. Sasa wewe shangilia kuishi Dar es Salama kwa maana hapa hakuna majambazi. Ila endelea na vitisho vyako vya kijinga uone kama Kagera haijakuita.”

Nabii Sanga alizidi kuzungumza kwa kujiamini. Baada ya dakika tano mrs Sanga akaletwa ndani humo. RPC akamkabidhi fumo ya kujaza. Baada ya taratibu hizo za kuweka dhamana kufika tamati, nabii Sanga akazungumza huku akimtazama RPC Karata kwa dharau.

“Nashukuru baba yangu”

“Mke wangu huna haja kumshukuru huyu. Raisi ndio aliye toa agizo la wewe kutoka”

“Kweli mume wangu?”

“Ndio”

Nabii Sanga akampiga busu la mdomoni mke wake.

“Kwaheri KARATA”

RPC Karata akamtazama kwa hasira nabii Sanga anaye anza kuelekea mkangoni mwa ofisi hiyo huku akiwa amemshika mkono mke wake.

“Ingekuwa ina pendeza zaidi kama ungeendelea kukaa na mke wako wa ndoa. Kuliko kupambana na vijana kwa ajili ya kugombania mabinti wadogo.”

Kauli hiyo ya RPC Karata ikaustua sana moyo wa nabii Sanga, akasimama na kumgeukia RPC Karata aliye achia tabasamu pana sana usoni mwake.

“Unasemaje wew?”

Nabii Sanga aliuliza kwa dharua kubwa sana.

“Ni hivi. Acha kumdanganya mke wako kwa kutembea na binti mdogo kama Magreth. Tambua kwamba Magreth ana mchumba wake anaitwa Evans na ana mpenda sana na wewe unachunwa mjini hapa mzeee hahahaaaahahaaaa……..”

Nabii Sanga akaanza kuvimaba kwa hasira. Mrs Sanga machozi yakaanza kumwagika usoni mwake kwani jambo alilo kuwa ana lihisi kumbe hata RPC ana lifahamu tena kwa mapana.




“Kijana una vuka mipaka, nitakupoteza”

Nabii Sanga alizungumza kwa hasira sana huku akimkazia macho RPC Karata.

“Hee!! Unanitisha ndani ya ofisini yangu na umesahau kwamba hapa ni wapi wewe? Upo kituo cha polisi na unaye zungumza naye hapa sio ispekta ni RPC wa mkoa mzima. Toka ofisini kwangu kabla majini yangu hayajabadilika na nikakusweka ndani. Sasa wewe nenda kajichanganye kama alivyo fanya mke wako katika kukuteka na majambazi wake mchwara. Alafu utajua kwamba hichi kiti sijakikalia bahati mbaya. Utafia jela na nikuambie jambo moja macho yangu yote yana waangalia nyinyi. Jichanganyeni”

RPC Katara alizunhgumza kwa kujiamini huku akimtazama nabii Sanga. Mrs Sanga akamshika mkono mume wake na taratibu wakaanza kuondoka eneo hilo.

“Huyu kijana amekuwa jeuri sana. Nitamuonyesha mimi ni nani?”

Nabii Sanga alizidi kuzungumza kwa hasira. RPC Karata mara baada ya kushuhudia gari la nabii Sanga likiondoka eneo hilo la polisi. Akatoa simu yake ya mkononi na kumpigia kijana wake anaye husika katika maswala ya upelelezi.

“Njoo ofisini kwangu”

“Sawa mkuu”

RPC Karata akarudi kwenye kiti chake na kukaa, huku akitafakari ni jinsi gani anavyo weza kumfwatilia nabii Sanga katika kila hatua atakayo piga. Kijana huyo mrefu na aliye valia nguo za kiraia, akaingia ofisini humo, akampigia saluti mkuu wake wa kazi, kisha akakaa kwenye kiti kilichopo mbele ya meza ya mkuu wake.

“Milinga kuna kazi hatari sana nina hitaji kukupatia kuanzia hivi sasa”

“Sawa mkuu. Ni kazi gani?”

RPC Karata akamgeuzia Milinga laptop yake na kumuonyesha video iliyo rekodiwa na kamera za barabarani katika eneo la Mwenge, zikionyesha jinsi gari ya mrs Sanga ikimgonga dereva bodaboda pamoja na abiria wake.

“Hiyo ni ajali ambayo ilisababishwa na mrs Sanga. Hawa watu wamekuwa wakitumia muamvuli wa dini katika kufanikisha mambo yao. Kama hapa unaweza kuona kwamba ana makosa makubwa sana, ila nimepewa oda kutoka ikulu ya kumuachia, ikiwa raia wa kawaida huwa ni lazima wakumbane na adhabu kali sana”

“Nahitaji kuanzia hivi sasa uwe karibu sana na hii familia. Ikiwezekana hata uokoke na utafute nafasi katika kanisa hilo. Hakikisha kwamba una fwatilia nyendo za nabii Sanga hatua by hatua”

“Sawa muheshimiwa. Ila nina weza kukuuliza swali?”

“Uliza tu”

“Hii kesi ina husiana sana na askari wa usalama wa barabarani. Je kuna jambo jengine tofuati na hili ambalo una hitaji nilifwatilie as person matter au ni kutokana na ajali na kupewa oda kutoka ikulu kumuachia huru?”

Nabii Sanga akashusha pumzi taratibu, kutokana ana muamini sana kijana huyu Milinga.

“Una kumbuka kuna siku nilitolewa hapa na walinzi wa Ikulu na nikapelekwa Ikulu?”

“Ndio nina kumbuka?”

“Unakumbuka juu ya swala la yule kijana Tomas ambaye tulikuwa tuna mtafuta?”

“Ndio nina mkumbuka na hadi sasa hivi hatujamtia nguvuni.”

“Basi ishu ilikuwa hivi. Yule kijana alikuwa ana mahusiano ya kimapenzi na mke wa nabii Sanga. Kutokana na utamu kolea wa mapenzi yao, walipanga njama za kumteka nabii Sanga na wakawatumia wale majambazi tulio waua”

“Nabii Sanga aliweza kulifahamu jambo hilo. Hivyo alinipa kazi ya kumuua Tomas na mimi ndio niliye mtorosha Tomas ndani ya kituo hichi pasipo hata askari yoyote kuweza kugundua. Nikiwa katika harakati ya kumuua, nabii Sanga alinipigia simu na nikiomba nimuachie huru.Ila kutokana na askari kugundua kwamba Tomas hayupo basi ilitubidi kuingia katika ule msako. Raisi Mtenzi unaifahamu historia yake vizuri, hivyo aliweza kujua fika mtu wa pekee aliye mtorosha muhalifu ni mimi. Raisi alinipa masaa ishirini na nne niwe nima mpata la sivyo nina stakiwa kijeshi”

“Ilibibidi kuwa muwazi kwa muheshimiwa raisi hivyo alinisamehe. Ila jambo baya sana alilo lifanya huyu mzee hakudhubutu hata kuniomba msamaha kwa kile kilicho tokea. Leo hii mara baada ya mke wake kuachiwa huru, ana nitisha na kuniambia kwamba ana nionyesha na ata hakikisha nina ondoka hapa Dar na kuepelekwa Kagera. Siwezi kuwa mwema zaidi ya hapo. Tafadhali hakikisha una nipatia siri zao nyeti kuhakikisha kwamba tuna muangusha”

“Sawa mkuu nime kuelewa. Nitaifanya kazi yako kwa asilimia mia moja”

“Nita shukuru, nina imani una fahamu ni wapi kwa kuanzia?”

“Ndio muheshimiwa hakuna tatizo”

Afande Milinga akaagana na RPC Karata na kutoka ofisini hapo, huku kichwani mwake akianza kupangilia mfumo mzima wa kazi yake jinsi utakavyo kwenda.

***

Julieth na Evans wakafika Mlimani City. Wakaingia katika duka la wauazaji wa bidhaa za apple. Dada aliye zungumza na Evans masaa mawili yaliyo pita akabaki akimshanga kwa jinsi alivyo fungwa bandeji hiyo mikoni mwake.

“Si ume toka hapa ukiwa mzima?”

“Wee acha tu dada yangu. Nimepata ajali hapo Mwenge”

“Jamani pole sana”

“Asante”

“Ni ajali ya nini?”

“Pikipiki”

“Umegongwa au?”

“Hapana nilikuwa kwenye pikipiki, tugagongwa na gari bwana”

“Pole sana kaka, yaani kweli binadamu tuna tembea na vifo mkonini”

“Wee acha tu”

“Simu yako si kama ile pale”

“Ndio”

Julieth akamnunulia Evans simu hiyo na Evans. Julieth akampigia simu baba yake ili kufahamu ni jambo gani linalo endelea.

“Tupo njiani tuna elekea nyumbani na mama yako”

“Sawa je gari langu vipi lime achiwa?”

“Sijafwatilia bwana mambo ya magari. Huyo mgonjwa wako ana endeleaje?”

“Amesha ruhusiwa hospitalini”

“Fidia ana taka nini?”

“Aha…sija zungumza naye kuhusiana na swala la fidia”

“Zungumza naye kisha urudi nyumbani sasa hivi”

“Sawa baba”

Julieth akakata simu, akamuomba Evans wakae kwenye mgahawa wa Samaki Samaki ili waweze kuzungumza mambo mawili matatu. Evans hakuwa na kipingamizi cha aina yoyote. Wakaagiza chakula na taratibu wakaanza kula.

“Ahaa baba ameniuliza kama kuna fidia ya aina yoyoye ambayo una weza kudai ili tukupatie”

“Hapana usijali. Kutokana simu yangu ime rudi hakuna tatizo”

“Kweli”

“Ndio Julieth”

Evans alizungumza huku akiendelea kuudadisi uzuri wa Magreth.

“Aha samahani Evans hapa mjini una jishuhulisha na shuhuli gani?”

“Nimemaliza chuo, nilipata matatizo ya kuvamiwa na vibaka na wakaniibia vyeti vyangu vyote”

“Aisee pole sana”

“Nashukuru”

“Sasa una ishije hapa mjini kama huna kazi?”

“Nimejishikiza kwa msichana mmoja ambaye ni mpenzi wangu. Japo ame nieleza kwamba ana mpenzi wake. Ila bado nina endelea kutafuta tafuta maisha si unajua wana wake muda wowote wana badilika”

“Ni kweli, sasa ina huyo mwanamke mpenzi wake yupo wapi?”

“Hajanieleza, japo ana kiri kwamba ana nipenda. Ila ndio hivyo maisha yake hayo ame tengenezewa na mwanaume wake”

“Pole sana Evans na ume somea maswala gani?”

“Nimesomea mambo ya biashara”

“Ahaa ngoja kuna kampuni ya usafirishaji nina hitaji kuifungua mwezi huu. Basi nita kupa nafasi ya umeneja”

“Kweli?”

“Haki ya Mungu. Nimeagizia roli ina ya Benz zipatazo hamsini. Zitakuwa zina chukua mizigo bandarini, kupelekea nje ya nchi”

“Aissee hongera sana. Je nina weza kukuuliza swali?”

“Uliza tu”

“Pesa zote hizo umezitoa wapi ikiwa una onekana ni binti mdogo”

“Wazazi wangu ni mabilionea. Wana pesa nyingi sana, hivyo waliniuliza ni mradi gani ambao ningependa kufanya. Nikaona ni heri nifungue biashara hiyo. Gari hizo zipo baharani na zina tokea nchini Ujerumani”

“Nashukuru kukutana na wewe na nina kuahidi kwamba nita simamia kampuni yako na itwa kwenda vizuri sana”

“Sawa kikubwa ni kujituma. Japo mmi ni mwanafunzi ila ni mfwatiliaji mzuri sana katika maswala ya pesa”

“Sinto kuangusha.”

“Kesho kama uta pata muda. Tukutane ili niweze kukupatia pesa ambayo una weza kupangisha nyumba ya kwako mwenyewe. Hapa nina fikiria endapo mwanaume huyo ata kuja kukukuta ndani ya nyumba ya demu wake ita kuwaje? Au hilo hujawahi kulifikiria?”

“Nimelifikiria ila mwanamke huyo ameniambia kwamba yupo tayari kupoteza kila kitu ili mradi awe na mimi?”

“Si kwa dunia ya sasa hivi. Ana kudanganya sana huyo mwamke, hakuna mtu ambaye ata kubali kuishi katika maisha ya umasikini kisa mwaume. Hapana amekuingiza cha kike na tena na kutafutia matatizo makubwa sana”

Maneno ya Julieth kidogo yakaanza kumpa wasiwasi Evans.

“Ila sijui lakini, ila kwa asilimia kubwa ya wanawake wa hapa mjini, hususani wale ambao wana wana pata wanaume wa kuwawezesha, wana mambo mawili. Yupo tayari kukufanya wewe kuwa kaka yake pale atakapo kuwa na mwanaume huyo au kukuacha kabisa. Kuwa makini sana Evans”

“Nimekuelewa dada yangu”

“Sawa muda wangu ni mdogo, acha niondoke hapa, niwahi nyumbani na pia nifanye taratibu za kulitoa gari langu polisi”

“Sawa nina shukuru kwa muda wako”

Julieth akafungua pochi yake na kutoa laki moja na kumkabidhi Evans.

“Kodisha taksi ikufikshe nyumbani. Angalia usije ukapanda pikipiki ukapata tena matatizo”

“Nina shukuru sana”

Wakaagana na Evans akaanza safari ya kurudi kigamboni, huku Julieth akirudi nyumbani kwa baba yake. Evans akajifikria kwa muda na kuona hakuna haja ya kurudi nyumbani muda hao. Moja kwa moja akaelekea kwenye mgahawa wa Magreth. Kwa bahati nzuri akamkuta Magreth aliye jawa na mshangao mara baada ya kumuona mume wake akiwa katika hali hiyo.

“Kuna nini kimekupata mume wangu”

Evans akamuelezea Magreth hali halisi ya tukio lilivyo tokea. Hakumuelezea kukutana na Julieth kwani ana imani kwamba kupitia msichana huyo basi ana weza kupata msaada mkubwa sana utakao mtoa kimaisha.

“Basi twende nyumbani uka pumzike”

“Wewe si upo kazini mpenzi wangu?”

“No ila hali yako sio nzuri, twende nyumbani sasa hivi uka pumzike”

Magreth alizungumza kwa msisitizo. Evans hakuwa na pingamizi lolote zaiid ya kukubaliana na mke wake huyo. Magreth akaacha majukumu yote ya kuendesha mgahawa huo kwa Juma, kisha yeye na Evans wakaondoka na kuianza safari ya kuelekea nyumbani kwao Kigamboni.

***

Nabii Sanga akafika nyumbani kwake huku akiwa amejawana hasira kali sana. Akapitiliza hadi chumbani kwake, akafungua shelf ya kuhifadhia nyaraka zake muhimu pamoja na bastola yake. Akachukua bastola yake na kuichomeka kiunoni kwa nyuma.

“Una kwenda wapi mume wangu?”

Mrs Sanga alizungumza huku akimtazama mume wake aliye fura kwa hasira.

“Sitaki maswali ya kipumbavu. Wewe hujaona udhalilishanji nilio pewa na yule kijana”

“Mume wangu, nakuomba uzuie hasira yako. Kumbuka kwamba wewe ni mtumishi wa Mungu mbele ya macho ya watu. Itakuwaje pale watu wakisikia kwamba ume fanya mauaji?”

“Sijali mimi, nita hakikisha kwamba nina mfundisha adabu. Ninakwenda na nikirudi hapa ninataka unipe majibu ya wapi ulikuwa unakwenda hadi uka gonga mtu. Umenielewa wewe mwanamke”

Nabii Sanga alizungumza kwa msisitozo huku akimtazama mke wake. Mrs Sanga hakuwa na uwezo wa kumzuia mume wake. Nabii Sanga, akafungua kabati linalo hifadhia kofia zake, akachukua moja ya kofia na kutoka ndani humo. Akabadilisha gari na kutumia gari aina ya BMW X6 ambayo ni mara chache sana amekuwa akiitumia. Kilicho mkasirisha nabii Sanga si dharau za RPC Karata, ila kitu kinacho muumiza moyoni mwake ni kuhusiana na mahusiano ya Magreth na Evans kijana ambaye alimsaidia hospitalini kwa kumlipia matibabu mara baada ya kuchomwa kisu na wahuni wa mtaani.

‘Lazima nimuue huyu ngedere. Hawezi kunichukulia mwanamke wangu ninaye mpenda’

Nabii Sanga alizungumza huku akizidi kuongeza mwendo wa gari lake.Akafika nyumbani kwa Magreth, akalisimamisha gari lake katika moja ya dula la karibu na nyumba hiyo. Akashuka na kuanza kutembea hadi getini kwa nyumba ya Magreth. Akatoa funguo za geti hilo na kufungua, akaingia ndani. Ukimya wa nyumba hiyo haukumuogopesha nabii Sanga. Akafungua mlango wa mbele wa nyumba, akaingia na kuufunga kwa ndani.

Nabii Sanga moja kwa moja akaeleka chumbani kwa Magreth na kuingia ndani,kitu kilicho mshangaza na kumuumiza roho yake ni kukuta nguo za mwanaume.

“Huyu malaya ana ujasiri gani wa kuishi na mwanaume ikiwa kila kitu hapa ni mali yangu?”

Nabii Sanga alizidi kuzungumza kwa hasira kali sana. Akaichomoa bastola yake na kukaa kitandani hapo huku akimsubiria Magreth na Evans kwa hamu sana.


Nabii Sanga akatazama kitanda hicho alicho kalia huku machozi yakimlenga lenga kwa uchungu sana. Kitanda ambacho alikuwa ana lalia na mwanamke anaye mpenda leo hii yupo mwanaume mwengine anaye lalia. Nabii Sanga akatazama jinziza kiume jinsi zilivyo jaa katika kabati la nguo la Magret huku zikichanganyikana na nguo za Magreth. Kelele za geti kufunguliwa, zikamfanya nabii Sanga kunyanyuka kwa haraka na kufungua la chumba hicho na kufungulia dirishani. Akawaona Magreth na Evans wakishuka kwenye gari hilo alilo wanunulia. Magreth akafunga geti hilo, ila kilicho mshangaza nabii Sanga ni bandeji aliyo fungwa Evans mkononi mwake.

Baada ya Magreth kufunga geti hilo, akamshika Evans kiuno na kuanza kuingia naye ndani. Nabii Sanga akatazama ni sehemu gani ambayo ana weza kujificha, kwa haraka akakimbilia bafuni huku bastola yake ikiwa mkononi.

‘Lazima nimwage mtu ubongo wake’

Nabii Sanga aliwaza huku bastola yake akiwa ameishika vizuri sana. Evans akaka kwenye moja ya sofa la sebleni hapo huku akijihisi mwili mzima kuchoka.

“Sijui yule dereva wa watu kama atakuwa hai”

Evans alizungumza huku akimtazama Magreth alieye fungua friji kubwa lililopp sebleni hapo.

“Tuta fwatilia taarifa zake. Mume wangu una uhakika kwamba dokta ame kueleza huja pata tatizo lolote kwa ndani?”

“Ndio, ni michubuko midogo midogo kwa maana ile ajali ilipo tokea. Nilirushwa mbele hivi, hivyo sikukubali kutua kama mzigo, ilinibidi kubingirika kitandani ili kuendena na ule msukuko nilio upata.”

“Mmmmm ila Mungu ame husika katika hilo kwa maana sasa hivi ungekuwa na majanga”

“Ni kweli, njoo hapa”

Evans alizungumza na Magreth akamfwata sehemu hiyo. Magreth akamkalia Evans mapajani mwake. Evans akamtazama Magreth kwa muda usoni mwake, kisha akampokonya glasi ya maji aliyo ishika na kuiweka mezani.

“Nini tena baby”

“Nina hamu na wewe”

Evans alizungumza huku akimgeuza Magreth na kumkalisha mkao ulio wafanya watazamane huku Magreth akiwa ameyakalia mapaja ya Evans. Kutokana Magreth leo alijiandaa kwa ajili ya kumburudisha nabii Sanga na akakosa huduma yake, hakuona haja ya kumnyima penzi Evans. Taratibu wakaanza kunyonyana lipsi zao huku kila mmoja akiwa amejawa na furaha kubwa sana. Magreth akamvua Evans tisheti aliyo ivaa na taratibu akaanza kupitisha viganja vyake kwenye kifua hicho.

‘Twende ndani baby”

Magreth alizungumza huku akihofia kamera zilizo fungwa sebleni hapo kwa pendekezo la nabii Sanga. Evans akambeba Magreth.

“Baby utaumia mkono”

“Hakuna cha kuumia mpenzi wangu”

Evans alizungumza huku akipiga hatua za kuelekea ndani ya chumba hicho. Wakaingia ndani na taratibu akamlaza Magreth kitandani huku akimnyonya shingo yake. Miguno ya kimahaba ya Magreth ikazidi kumchanganya nabii Sanga. Hakuamini maishani mwake kama ipo siku Magreth atakuja kumsaliti. Nabii Sanga akafungua mlango wa bafuni humo taratibu na kuchungulia kitandani. Akamuona jinsi Magreth anavyo nyonywa maziwa yake kwa fujo Evans.

Nabii Sanga akafungua kwa nguvu mlango huo na kutoka chumbani hapo na kuwafanya Evans na Magreth kukurupuka na kuacha hicho wanacho kifanya. Macho yakamtoka Magreth huku mapigo yake ya moyo yakimdunda kwa kasi sana. Nabii Sanga akavua kofia hiyo na kumfanya Evans aweze kumfahamu mzee huyo, ukiachilia umaarufu wake wa kuwaponya watu, ila ni mzee ambaye alimsaidia katika matibabu yake.

“Mage Mage Mage. Huyu ndio panya anaye kufanya una nisaliti mimi?”

NabiiS anga alizungumza kwa hasira sana huku akimtazama Magreth aliye chukua mto na kujiziba maziwa yake huku mwili mzima ukimtetemeka kwa woga.

“Kijana huyu hakukuambia kwamba mimi ni mume wake?”

Evans akamtazama Magreth aliye anza kumwagikwa na machozi yatokanayo na woga. Nabii Sanga akaunyanyua mkono wake ulio shika bastola na kumuelekezea Evans usoni mwake.

“Ninakuua humu humu ndani alafu hakuna mjinga yoyote ambaye ata jua juu ya uwepo wako. Fala wewe”

Nabii Sanga alizungumza huku bastola hiyo ikiwa ime lenga kichwa cha Evans amabye naye yupo kwenye wakati mgumu. Woga ume mtawala mwili mzima, leo ana amini ndio mwisho wa maisha yake, kwani kama aliponyoka ponyoka kufa kwa kugongwa na gari basi haamini kama ana weza kutoka mikononi mwa nabii Sanga.

“Mu..me wa…ngu nakuomba u…u…msamehe Evans”

“Funga bakuli lako malaya wewe. Nikupe nini eheee, nimefanya kila liwezekanalo kwa ajili yako, ila haya ndio matusi ya maliyo yako eheee?”

Nabii Sanga alizidi kufoka kwa hasira sana.

“Shuka kitandani kenge wewe”

Taratibu Evans akatii amri hiyo na kushuka kitandani huku miguu yake ikiendelea kumtetemeka.

“Huwa sinaga huruma na watu wanao jaribu kuchovya vidole katika mzinga wangu wangu wa asali”

Nabii Sanga alizungumza huku akimuelekezea Evans bastola ya kichwa tayari kwa kumfumua ubongo wake.

***

“Tomas mume wangu, hivi kuna haja yoyote ya sisi kuondoka hapa Afrika kusini kuelekea Nigeria?”

Mke wa Tomas alizungumza huku akwia amekilaza kichwa chake kifuani mwa mume wake.

“Itabidi kwa maana kuna endapo askari wakafanya upelelezi na kufahamu kwamba tume muua yule jamaa ita kuwaje?”

“Ni watu wangapi huwa wana uwawa hapa Afrika kusini na hakuna sheria zinazo chukuliwa dhidi yao. Kwenye hii nyumba mimi nina jiona tupo salama”

“Sawa nita jaribu kumshawishi ndugu yangu. Akiona ina faa basi tuta endelea na maisha yetu hapa. Ila ni lazima tuangalie ni nii cha kufanya na tusiwe tuna ishi na kuwa tegemezi kwa mtu”

“Sawa mume wangu. Nipo tayari kukuunga mkono katuka jambo lolote ambalo una lifanya mume wangu”

“Kweli?”

“Ndio”

Taratibu Tomas akaanza kunyanyana ndimi na mke wake. Kutokana wote wapo kama walivyo zaliwa, ikawa ni rahisi sana kwa kuanza mtanange huo wa kukata na shoka. Ndani ya dakika hamsini, kila mtu akwa amesha ridhishwa na mwezake. Tomas akashuka kitandani mara baada ya mke wake kupitiwa na usingizi, akavaa nguo za kulalia ambazo walizinunua madukani. Akatoka chumbani humo na kuingia katika chumba walicho mlaza mtoto wao na kumkuta akiwa amelala. Akaelekea selbeni na kumkuta Ngosha akitazama filamu.

“Vipi huja lala kaka?”

“Yaa usingizi haupandi kabisa.”

“Kwa nini?”

“Mmmm nawaza mambo mengi sana. Unajua hili genge ninalo limiliki nina ona nilisambaratishe.”

Ngosha alizungumza kwa upole huku akimtazama Tomas usoni mwake.

“Kwa nini kaka, ikiwa wana kuletea faida kubwa?”

“Ni kweli, ila wao pia wana maisha. Wana taka kutengeneza familia kama wewe, unajua uwepo wa mke wako na mtoto wako humu ndani. Nimeona mabadiliko makubwa sana kwenye moyo wangu na mimi pia nina bidi niwe na familia. Umri una kwenda kaka na hizi mali zote endapo ikitokea nikafariki nani ata kuwa ni mridhi?”

Ngosha alizungumza kwa msisitizo huku akimtazama Tomas usoni mwake.

“Unahisi vijana wako wata hitaji kutawanyika?”

“Ndio jambo ambalo nina liwazia.”

“Ila ngoja nikushauri kitu”

“Nishauri ndugu yangu”

“Hii nchi sio chimbuko letu. Una pesa nyingi sana kwa nini usiende kuwekeza Tanzania. Kuna kesho na kesho kutwa, itatulazimu kuondoka katika hii nchi hii. Pesa tunaweza kubeba je majumba”

“Ni kweli ndugu yangu. Unajua toka bi mkubwa afariki nchini Tanzania, nimekuwa ni mtu wa kuitenga sana ile nchi. Ndugu wote walio baki, waling’ang’ania mali na mimi niliamua kujitafutia za kwangu na mwishowe nasikia wame kula mali zote na wame fulia”

“Sawa ndugu ila huwekezi kwa ajili yao. Ila una wekeza kwa ajili ya kizazi chako.”

“Niushauri mzuri sana ndugu yangu. Nitaufanyia kazi”

“Nashukuru kwa hilo. Eheheee!! Shemeji yako amenishauri kwamba ikiwezekana tuendelee kuishi tu hapa nchini Afrika kusini. Hakuna haja ya kuelekea nchini Nigeria”

“Kwa nini ameshauri hivyo ikiwa kuna mauaji yalitokea pale ndani?”

“Ni kweli, ila kwa jinsi vijana wako walivyo fanya usafi na kusafisha eneo lile sidhani kama kuna polisi ana weza kugundua kama ndani ya nyumba ile kume tokea mauaji”

“Sawa kama ndio anavyo hitaji. Je upo tayari kuifanya ile biashara ya kuchukua wanawake nchini Tanzania na kuwaleta huku kwa ajili ya bishara?”

“Nitalifikiria hilo”

“Sawa je biashara ya unga au nimueleze Adela kwamba una hitaji muda zaidi?”

“Nipe wiki moja kaka nita kupatia jibu”

“Sawa ndugu yangu. Hivi Tanzania ni biashara gani ina lipa zaidi kwa maana wewe kule ulikuwa dalali na una fahamu watu wengi”

“Ukifungua kumbi za Starehe na kumbi za maharusi. Uatapata pesa nzuri sana”

“Basi katikati ya wiki hii nitakwenda nchini Tanzania kuhakikisha kwamba nina fanya upelelezi wangu wa kutosha na kuhakikisha kwamba nina fungua biashara nzuri sana ambayo ita lipa”

“Sawa kaka, nami nina tamani sana kurudi nchini humo ila yale majanga yana weza kuni kumba tena”

“Usijali, nitafanya upelelezi wa jambo lako nan ita kuambia ni ninikinacho endelea”

“Poa kaka, ila yule mjinga nabii Sanga hakikisha una nijia na full data zake. Yaani nitahitaji kumuua kwa mikono yangu mimi mwenyewe”

Ngosha akamtazama Tomas kwa umakini sana kisha akamnyooshea dole gumba akimaanisha kwamba ata lifanyia kazi jambo hilo.

***

“Mama yupo wapi?”

Julieth alimuuliza dada wa kazi.

“Yupo chumbani”

Julieth akapandisha gorofani, akasimama mlangoni mwa chumba hicho cha wazazi wake. Akaanza kugonga tartaibu.

“Nani?”

“Mimi mama”

“Ingia”

Julieth akaingia na kumkuta mama yake akiwa amelala kitandani. Taratibu Julieth akaka pembeni yake huku akimtazama usoni mwake.

“Mama una jisikiaje?”

“Vizuri”

“Kesi ime kwisha?”

“Hapana wameniachia kwa dhamana ila itanibidi kuripoti polisi kesho”

“Ila una jisikiaje?”

“Nina mawazo mengi sana na nikweli baba yako ana mahusiano na Magreth”

“Umejuaje mama?”

“RPC alizungumza mbele yetu kwa maana kulitokea kuto kuelewana kati ya baba yako na RPC”

“Sasa mama uta mfanya nini Magreth”

“Kosa sio la kwake. Kosa ni la baba yako.”

Mrs Sanga alizungumza kwa sauti iliyo jaa masikitiko makubwa sana.

“Ila sinto muacha salama huyu binti ni lazima nidili naye. Nita hakikisha nina muua kwa mikono yangu mimi mwenyewe.”

“Mama!”

“Ndio lazima nifanye hivyo na wewe nina kufundisha kwenye maisha yako. Usiruhusu mwanamke mwengine akakchukulia mwanaume wa maisha yako. Hususani mume uliye funga naye ndoa. Hakikisha kwamba una pigania ndoa yao hadi dakika ya mwisho. Una nielewa?”

“Ndio mama”

“Kwanza una mchumba?”

“Sina”

“Ulisha wahi kupenda?”

“Hapana mama, kama ninge penda. Ningekueleza wewe ndio msiri wangu”

“Sawa. Baba yako alihidi akirudi ata hitaji kufahamu ni wapi tulikuwa tuna elekea. Hakikisha hufungui kinywa chako kumueleza tuliyo yafanya leo ume nielewa?”

“Usijali mama katika hilo. Nahitaji kulitoa gari langu je nifwate hatua gani?”

“Mmmm wasilana na mwanasheria wa familia. Ana weza kukusaidia katika hilo”

“Sawa mama cha nifanye hivyo”

Julieth alizungumza huku akitoka ndani humo kwa mama yake. Akawasiliana na mwanasheria wa familia na kumuomba aweze kufika nyumbani hapo.

***

Magreth akajikaza na kushuka kitandani hapo huku akiendelea kulia kwa uchungu. Taratibu akapiga magoti pembeni ya nabii Sanga na kuishika miguu yake yote miwili.

“Sanga mume wangu nina kuomba nisamehe. Sinto rudia kufanya kosa hili tena”

Magreth alizungumza kwa uchungu sana. Maneno ya Magreth yakamuumiza sana Evans moyo wake, akayakumbuka maneno ya Julieth kwamba hakuna mwanamke hapa mjini ambaye ana weza kusaliti mali kwa ajili ya mapenzi.

“Mimi na huyu panya hapa una mpenda nani?”

Magreth taratibu akamtazama Evans kisha akamtazama nabii Sanga aliye ishika bastola yake aliyo muelekezea Evans bastola hiyo.

“Nakupenda wewe tu Sanga. Kumbuka kwamba wewe ndio mwanaume wangu wa kwanza kunitoa usichana wangu. Kumbuka hata leo nimeshinda kukupa penzi kule hotelini hii yote ni kutokana na tatizo lililo jitokeza. Nisamehe mume wangu nakupenda sana”

Maneno ya Magreth yaka mnyong’onyeza sana Evans, akajikuta akijuta ni kwa nini amemfahamu Magreth na kufanya mambo yote ikiwemo la kumsaidia kumuokoa kutoka mikononi mwa vibaka ambao mwishowe aliambulia kuchomwa kisu na chupuchupu afariki dunia.


Maneno ya magreth kidogo yakamfariji nabii Sanga na kuiyayusha hasira yake ambayo imevuka kiwango chake cha kwaida.

“Wewe mbwa, nikifumba macho na kufumbua nina kuhitaji uwe ume potea ndani humu”

Evans hakutarajia kupata nafasi kama hiyo. Kwaharaka akatoka chumbani hapo, alicho kikumbuka kukichukua sebleni ni boksi lenye simu yake pamoja na tisheti aliyo kuwa ameivaa. Akatoka kwa kasi katika nyumba hiyo ya Magreth na kutoweka kabisa katika mtaa huo kwani akionekana basi ana weza kuuwawa na nabii Sanga. Nabii Sanga taratibu akachuchumaa huku akimtazama Magreth usoni mwake, akamkumbatia huku akimpiga mabusu mfululizo.

“Yaani ingekuwa sio wewe. Ningemuua yule mshenzi, hawezi kukuchukua kirahisi rahisi”

Nabii Sanga alizungumza kwa majigambo. Akamnyanyua Magreth na kumlaza kitandani, haraka haraka akavua nguo zake, akaitanua miguu ya Magreth ambaye bado ana endelea kulia na kujutia kuzungumza maneno ambayo ana amini kwa namna moja ama nyingine yame muumiza sana Evans. Ila kwa upende mmoja amefanya hivyo ili mradi kuyaokoa maisha ya Evans ambayo yalikuwa yapo hatarini sana kupote. Nabii Sanga hakujali Magreth yupo kwenye hali gani ila alicho kifanya ni kuhakikisha kwamba ana kata kiu yake ambayo ni kwa muda mrefu sana ilikuwa ina mkabili.

***

Evans akafika katika kituo cha daladala huku akiwa haamini kama yupo hai. Katika maisha yake hii ndio mara yake ya kwanza kunyooshewa bunduki tena kwa lengo la kuuwawa.

‘Niende wapi mimi?’

Evans alijiuliza huku akiendelea kushangaa dalala zinazo simama na kuondoka katika kituo hicho. Kutokana kwenye wallet yake kuna pesa ya kutosha, akakodisha bajaji ikampeleka hadi maeneo ya Kinondoni, akapangisha chumba katika hoteli ya Nemax. Akatoa simu hiyo iliyopo kwenye boksi, akaiweka chaji. Akajizala kitandani huku akeindelea kuyafikiria maneno ya Magreth.

“Ina bidi ni move on”

Evans alizungumza huku akijizungusha zungusha kitandani.

‘Daa simu line yangu nime iacha kwa huyu mshenzi. Ila hakijaharibika kitu nita tafuta line nyingine na sinto hitaji niwe na mawasiliano naye kabisa’

Evans aliendelea kupanga mikakati yake. Siku nzima hakutoka nje ya chumba hicho na aliagiza chakula ndani humo humo. Asubuhi na mapema, akamuazima mmoja wa wahudumu simu yake kwa ajili ya kuwasiliana na Julieth. Akaiingiza namba ya Julieth katika simu ya mhudumu huyo na kuiweka sikioni mwake. Simu ikaita na baada ya muda ikapokelewa.

“Habari za asubuhi”

“Salama nani mwezangu”

“Evans”

“Ohhoo Evans mbona ume tumia namba mpya?”

“Yaa kuna matatizo kidogo niliyapata. Imenilazimu kuazima simu ya mtu hapa nilipo”

“Matatizo gani na upo wapi?”

“Nipo Nemax Hotel”

“Hapo Kinondoni?”

“Ndio”

“Basi nina kuja sasa hivi”

“Sawa nipo chumba namba mia na kumi na tano”

“Sawa nina kuja”

“Hii ni namba ya muhudumu wa hapa hotelini”

“Sawa usijali”

Evans akakata simu na kumrudishia muhudumu huyo wa kike. Akampatia noti ya shilingi elfu kumi kama asante yake na kurudi chumbani kwake. Halikuisha hata lisaa moja Julieth akafika hotelini hapo huku akiwa amevalia kofia ambayo ime uficha uso wake kwa asilimia kubwa sana. Akafika katika chumba cha Evans akagonga na kufunguliwa mlango. Evans akamkatibisha, wakasalimiana kwa kumbatiana kisha Julieth akaka kwenye moja ya sofa.

“Samahani sana kwa kukusumbua asubuhi asubuhi hii”

“Usijali ni mambo ya kawaida. Ehee niambie ni nini kimetokea?”

“Mume wa yule demu alifika jana nyumbani. Yaani nimeponea chupuchupu bado nusu tu aniue kwa kunipiga risasi”

“Jamani”

“Ndio hivyo dada yangu”

“Pole sana Evans. Ila jana nilikuambia, umeona sasa. Hayajapita hata masaa ishirini na nne, kile nilicho kisema kimekuwa”

“Ndio hivyo”

“Pole hapa ume chukua chumba kwa muda gani?”

“Siku na saa nne ina nibidi kuondoka”

Julieth akafungua pochi yake na kutoa kiasi cha laki tatu na kumkabidhi Evans.

“Ongeza muda wa kukaa hapa hotelini. Nina kwenda polisi asubuhi hii na mwana sheria wangu kwenda kuitoa gari yangu. Baada ya hapo tuta wasiliana tujue ni wapi tuna anzia katika kutafuta nyumba ya kuishi”

“Nashukuru sana Julieth”

“Usinishukuru. Hivi ni vitu vya kawaida tu”

Julieth alizungumza hukua kiachia tabasamu pana usoni mwake. Ukweli ni kwamba jana usiku Julieth hakuweza kupata hata lepe usingizi kwa kumuwaza Evan. Kwenye maisha yake ametongozwa na wanaume wengi sana ambao wengi wao wana mfwata kwa ajili ya uzuri na utajiri wake. Ila kati ya wanaume hao wote hakuwahi kumpenda wala kumjibu hata mmoja wao. Ila kwa Evans amejikuta moyo wake ukiachanua kwa hisia kali za kimapenzi kwa kijana huyo ambaye ame kutana naye kwenye ajali tu.

“Nimefunzwa kushukuru kwa kila jambo hivyo usishangae kwa mimi kushukuru kwangu”

“Sawa Evans, acha mimi niwahi polisi centra. Ila nakuomba ufanye jitihada za kusajili laine yako”

“Nimepoteza vitambulisho vyangu, yaani hapa nilipo nipo mimi kama mimi”

“Oohoo basi nita kusajilia. Una penda kutumia voda au tigo?”

“Tigo”

“Basi nitakuletea. Hakikisha huondoki hapa hotelii hadi nitakapo rudi”

“Usijali”

Julieth akamtazama Evans kwa muda. Akatamani kumuambia jambo ila akashindwa kabisa na kujikuta akiondoka pasipo kuzungumza ukweli wa hisia zake.

***

Hadi ina timu saa moja asubuhi Magreth hakuweza kupata hata lepe la usingizi. Mizunguko yote minne aliyo ienda nabii Sanga, hapakuwa na mzuko hata mmoja ambao uliweza kumridhisha kimapenzi. Hisia na akili zake wala hazipo kwa mzee huyo anaye koroma pembeni yake. Magreth akashuka kitanda, akachukua simu yake na kutoka ndani humo. Akanza kuitafuta namba ya Evans na kumpigia, ila kila alipo jaribu kufanya hivyo hakuweza kumpata hewani. Furaha ikazidi kupotea Magreth kwani mwanaume anaye mpenda ndio hivyo amesha utibua moyo wake.

‘Ehee Mungu nita fanya nini mimi?’

Magreth alilalama huku machozi yakimwagika usoni mwake. Akarudi chumbani na kumkuta nabii Sanga akijigeuza geuza.

“Baby”

Magreth alimuita nabii Sanga haku akimtingisha tingisha.

“Mmmm”

“Kume pambazuka. Amka”

“Saa ngapi hivi sasa?”

“Mbili kasoro asubuhi”

Nabii Sanga akajinyoosha viongo vyake huku akipiga miyayo mfululizo.

“Huja kwenda kwako, ita kuwaje kw make wako”

“Achana naye hana jambo la kunieleza”

Nabii Sanga alizungumza huku akishuka kitandani hapo. AKajisaidia khaja ndogo na kurudi chumbani.

“Leo nahitaji unipikie chakula kizuri sana na nita lala hapa hapa hadi kesho”

“Kesho?”

“Ndio una shangaa nini? Au una hitaji yule mjinga wako aweze kurudi hapa?”

“Hapana”

“Ila?”

“Nisamehe mumewangu. Kumbuka nina mgahawa wa kusimamia”

“Wewe kaa nyumbani hapa kwa maana kama ni huo mgahawa si nime ume ufungua kwa pesa yangu?”

“Ndio”

“Basi hata wateja wasipo kuja nita kulipa hicho kiasi unacho ingiza kwa siku”

Nabii Sanga alizdi kujiamini kwani ana nguvu kubwa sana ya pesa ambayo ina muwezesha kumshawishi mtu yoyote kwa kila jambo analo lihitaji.

***

Mrs Sanga hakuweza kumuona mume wake hadi kuna pambazuka. Wasiwasi ukaanza kumjaa kwa maana kila anapo jaribu kumpigia simu, hampati hewani. Mrs Sanga akafikiria ni eneo gani ambalo mke wake ana weza kuwepo, kwani kuondoka na bastola yake jana mchana sio jambo la kawaida.

‘Au atakuwa amekwenda kwa yule malaya wake?’

Mrs Sanga aliwaza huku akijaribu kuunganisha matukio ya siku iliyo pita. Akaikumbuka kauli ya RPC Karata, aliye mshutumu kwa kutembea na msichana mdogo amabye ana mpenda mpenzi wake ambaye ana itwa Evans.

“Pumbavu sana huyu mwanaume”

Mrs Sanga alizungumza huku akikurupuka kitandani hapo. Akaingia bafuni na kuoga haraha haraka, akajiandaa na kuondoka nyumbani hapo kwa kutumia gari lake. Breki yake ya kwanza akafika katika Mgahawa wa Magreth. Akasimisha gari lake kwenye maegesho, aikaitazama saa yake ya mkononi na ina muonyesha ni saa mbili asubuhi.

Akashuka kwenye gari lake hili, huku akiiweka vizuri miwani yake. Akaangaza pande zote za mgahawa huo na kutafuta kiti ambacho hakina mtu na akaketi.

“Karibu sana mama”

“Nashukuru nina weza kupata kifungua kinywa”

“Ndio mama. Vyakula vyetu ni kama hivyo vilivyo andikwa kwenye hiyo menu”

Mrs Sanga akachukua kitabu hicho kilicho andikwa aina ya vyakula. Akachagua chai ya maziwa na yai moja pamoja na chapatti moja. Muhudumu huyo akaondoka na mrs Sanga akaendelea kuchunguza kila mtu anaye ingia na kutoka katika mgahawa huo. Muhudumu huyo akalete akaleta chakula hicho kabla ya kuondoka mrs Sanga akamzuia.

“Samhani, bosi wenu yupo wapi?”

“Aha…hajafika bado”

“Huwa ana fika kazini saa ngapi?”

“Mmmm huwa ni saa kumi na mbili. Ila toka alivyo ondoka jana mchana hakuweza kurudi labda nimuite meneja msaidizi aweze kukupa maelezo zaidi”

“Nitashukuru mwanangu”

Dada huyo akaondoka na baada ya muda akarudi akiwa ameongozana na Juma.

“Mama meneja msaidizi ndio huyu hapa”

“Sawa asante. Samahani kijana”

“Bila samahani mama yangu”

“Bosi wenu Magreth nina weza kumpataje kwa maana hadi sasa hivi nime ambiwa hajafika kazini”

“Ni kweli bosi jana aliondoka na mume wake mida ya mchana na mume wake alikuwa ana umwa”

“Ohoo kwa hiyo leo kuna uwezekano mkubwa wa yeye kuto kufika ofisini?”

“Sijajua kwa maana bado sija wasiliana naye”

“Hambu jaribu kuwasiliana naye ili ikiwezekana niweze kuonana naye kwani nina shida naye muhimu sana”

“Ni shida binafsi au shida ya kiofisi?”

“Ya kiofisi sana.Ila itakuwa ni vizuri sana kama nita zungumza naye mimi mwenyewe”

“Sawa, je nina weza kufahamu shida hiyo katika ofisi ina husian ana nini?”

Mrs Sanga akaka kimya kwa sekunde kadhaa huku akitafakarini ni jambo gani ambalo ana weza kumdanganya kijana huyo.

“Nahitaji kumpa tenda ya kutuletea chakula cha mchana ofisini kwangu. Nina wafanyakazi mia tatu hivyo una weza kuona kwamba ni oda kubwa sana hiyo. Nivyema nika zungumza naye uso kwa uso”

Juma kusikia ofa hiyo akajikuta akipagawa kwa furaha. Akampigia simu Magreth na baada ya sekunde kadhaa simu hiyo ikapokelewa.

“Bosi habari yako”

“Salama Juma vipi hapo kazini”

“Mambo yanakwenda safi sana bosi. Kuna mama mmoja hapa ana hitaji kuonana na wewe, ana hitaji kutupatia tenda ya kuwahudumia wafanyakaiz wake wa kampuni zaidi ya mia tatu”

“Mia tatu kwa kila siku au?”

“Eti mama ni wafanyakazi mia tatu kwa kila sikua au?”

“Ndio kuanzia juma tatu hadi juma mosi”

“Amesema kuanzia juma tatu hadi juma mosi. Hivyo ana hitaji kukutana na wewe ili muweze kuzungumza uso kwa uso ni jinsi gani muna weza kukubaliana juu ya oda hii”

Magrerth akakaa kimya huku akitafakari nini la kumjibu Juma.

“Kutokana leo siwezi kutoka nyumbani. Basi nina kuomba uweze kumleta nyumbani kwangu. Sawa”

“Sawa boss”

Juma akakata simu na kumtazama Mrs Sanga kwa tabasamu pana sana.

“Amesema twende nyumbani kwake. Je una weza kukubaliana na hilo”

“Hakuna tatizo, nina usafiri wangu na tuna weza kwenda.”

Mrs Sanga alizungumza kwa furaha kwani lengo la kwenda kwa Magreth sio hizo oda za chakula kwa wafanyakazi wake. Lengo la kwanza ni kupafahamu kwa adui yake huku akiamini kwa asilimia kubwa sana mume wake ata kuwepo nyumbani kwa Magreth.



Mrs Sanga wakaingia ndani ya gari hilo na wakaanza kuelekea nyumbani kwa Magreth.

***

“Ni nani umemuambia aje nyumani kwako?”

Nabii Sanga alimuuliza Magreth mara baada ya kutoka sebleni.

“Ni mfanyakazi wangu wa mgahawani alinipigia na kunieleza kuna mteja ana hitaji oda ya chakula katika kampuni yake na ana wafanyakazi mia tatu”

“Waoo ni good deal”

“Yaa ndio maana nime waeleza waweze kufika hapa kwa maana muhusika ana hitaji nizungumze naye uso kwa uso”

“Ni jambo zuri ila sio jambo zuri kumkaribisha mtu usinye mfahamu nyumbani kwako. Chakufanya waambie mukutane kwenye hoteli yoyote hapa Kigamboni, nina imani itakuwa ni jambo zuri na rahisi. Isitoshe mimi pia nipo hapa nyumbani, sinto penda watu waje kunikuta hapa au kukuta gari langu hapa. Umenielewa”

“Nimekuelewa mpenzi”

Magreth akampigia Juma simu na kmuomba waelekee kwenye hoteli ya Double Z na watakutania hapo.

“Sawa bosi”

Juma alijibu na simu ikakatwa. Magreth akaelekea bafuni, akaoga huku kichwa chake kikiwa na mawazo mengi sana juu ya Evans. Anatamani sana kuendelea na mahusiano na Evans, ila kila akikumbuka alipo toka kwenye ufukara wa kutembeza maandazi mtaani, ana jikuta akikata tamaa kabisa ya kuweza kukubaliana na swala la kuwa na Evans kwa mana hatamani kabisa kurudi chini. Magreth akajiandaa vizuri na kutocha chumbani humu. Akamkuta nabii Sanga akitazama kipindi chake kinacho rushwa kwenye televishion.

“Mage hivi kwa nini uliacha kuimba kwaya ya kanisani kwangu?”

“Mmmm kipindi kile majukumu yalikuwa ni mengi. Biashara ilikuwa ngumu sana, hivyo utakuta nikitoka kutembeza maandazi huwa nina choka sana na mwishowe nikaona hakuna jinsi zaidi ya kuachana na kazi hiyo”

“Basi wewe nenda huko alafu ukirudi tuzungumze juu ya swala la kuimba kwako. Natamani kukuona ukiimba wewe kama wewe, ukatoa albamu zako na kuuza, hiyo itakuwa ni njia moja yawapo nzuri ya kukuza kipawa chako, jina lako na ukazidi kutanuka kiuchumi”

Maneno ya nabii Sanga yakaanza kumfurahisha Magreth ambaye kwa sasa tamaa ya umaarufu na pesa ndio vimemkaa moyoni kuliko hata upendo wa dhati kati ya nabii Sanga na Evans.

“Sawa mume wangu”

Magreth akambusu nabii Sanga mdomoni mwake kisha akatoka ndani humu. Akingia ndani ya gari lake na kuianza safari ya kuelekea katika hoteli hiyo.

Mrs Sanga akambidi kukubaliana na ombi la Juma, wakafika katika hoteli hiyo, wakakaa sehemu nzuri na kuagizia vinjwaji.

“Pale kwenye mgahawa wenu kwa siku muna weza kupata wateja wangapi?”

“Mmmm….wengi sana”

“Kwa kukadiria wana weza kufika wangapi?”

“Elfu moja na miatano hadi elfu mbili.”

“Aisee kumbe muna watu wengi hivyo?”

“Yaa kuna kipindi wana kuwa hawatoshi pale. Hivyo nina mpango wa kumshauri boss kununya sehemu ya juu katika lile gorofa, ili kama ni watejawengine basi waweze kukaa juu”

“Ni kweli, kwa idadi hiyo ya wateja ina bidi kuongeza eneo”

“Yaa”

“Je mume wa bossi wako una mfahamu?”

“Ndio nina mfahamu ni kijana mmoja hivi. Jamaa yupo very smart na endapo boss ata endelea kuwa na yule jamaa basi nina asilimia mia moja wata fika mbali sana”

Simu ya Juma ika ita, akaitazama na kukuta ni Magreth, akaipokea na kumuelekeza sehemu walipo kaa. Magreth akaingia ndani ya hotele hiyo, akaanza kuelekea sehemu alipo kaa Juma na mwana mama huyo aliye mpa mgogo na kushindwa kuiona sura yake. Magreth akafika sehemu hiyo, akamsalimia Juma kwa furaha, kitendo cha kukutanisha macho yake na mrs Sanga, akastuka kidogo hadi Juma akahisi kuna jambo.

“Habari yako binti?”

Mrs Sanga alianza kusalimia huku akitengeneza sura iliyo jaa tabasamu pana usoni mwake. Magreth akabaki akiwa amesimama huku akiwa amejaa na mshangao, kwani ana mfahamu mrs Sanga vizuri sana.

“Bosi una salimiwa au kuna tatizo”

“Aha…ha…hapana. Salama”

Magreth alishikwa na kigugumizi.

“Karibu ukae”

Mrs Sanga alizungumza na taratibu Magreth akakaa hukua kimtazama mrs Sanga usoni mwake.

“Kijana una weza kutupisha nika zungumza na bossi wako?”

“Ndio hakuna shaka”

Simu ya Magreth ikaanza kuita, akaitoa kwenye pochi yake. Akaona jina la dada Vivian, akaitazama kwa sekunde simu hiyo kisha akaipokea.

“Mage habari yako”

“Salama dada”

“Mbona upo kimya toka juzi huja tujibu, kuna tatizo?”

“Nisamehe sana dada yangu, mume wangu alipata ajali. Ila nitakupigia nina kikao kidogo hapa”

“Ohoo pole sana ana endeleaje?”

“Ana endelea vizuri. Mungu ana saidia”

“Sawa hakikisha leo una wasiliana na mimi kwa maana baba ana ulizia ume fikia wapi, hivyo nina shindwa kumpatia jibu”

“Usijali dada yangu”

Magreth akakata simu na kutazamana na mrs Sanga ambaye sura yake iliyo kuwa na tabasamu ime potea. Magreth akashusha pumzi kidogo na kujiamini kwa kujibu chochote ambacho ata ulizwa na mwana mama huyo.

“Nimekuja kwa jambo moja tu na nina hitaji uni sikilize vizuri wewe mwanamke. Achana na mume wangu na endapo uta endelea naye nita kuua kwa mkono wangu mimi mwenyewe ume nilewa?”

Mrs Sanga alizungumza kwa sauti ya chini iliyo jaa msisitizo na wao wawili tu ndio wana weza kuisikia.

“Hahaaaa….samahani. Umechanganyikiwa mama?”

“Sijachanganyikiwa, nina ushidi wa wewe kutembea na mume wangu. Sasa achana naye na kama una hisi kwamba uta endelea kuvuna pesa za familia yangu. Haki ya Mungu tambua kwamba ume kosea kuingia kwa mwanaume wa mtu. Leo nina zungumza ila siku nyingine nita ongea kwa vitendo”

Magreth akatabasamu huku akimtazama Juma aliye kaa meza ya pili kutoka hapo walipo keti.

“Hivi unajua kwamba sikuogopi. Pili hivi una tambua kwmaba mimi ndio niliye warekodi mukifanya uchafu ofisini kwa mume wako tena kanisani. Unajua ile video bado ninayo kwenye simu yangu ya zamani. Hivi una tambua nikihitaju kuisambaza mitandaoni jinsi ulivyo kuwa ukifir** na Tomas dunia nzima ita jua uozo wa maisha yako. So usinitishe kama ni kisu mimi nimeshika makali na wewe na mumeo mume shika makali, nikihitaji kuvuta basi muta poromoka kama embe linavyo toka juu na kuanguka chini. Sawa mrs Sanga”

Magreth alizungumza kwa kujiamini huku akimkazia macho mrs Sanga aliye anza kumwagikwa na jasho huku wasiwasi mwingi ukiwa ume mjaa. Hakuwahi kuwazia kama binti huyo ambaye kipindi cha nyuma amekuwa ni muumini wa hali ya chini, leo hii ana mtisha kiasi hicho.

“Kutokana ulimteka mume wako wewe mwenyewe. Basi nina kueleza ukweli, nita mchuna hadi pale nitakapo ridhika na pesa atakazo kuwa amenipatia kisha nitakurudishia makapi. Siku nyingine usije kijinga jinga nita kufundisha adabu na ole wako ujidanganye kutuma watu kama ulivyo mtumia mume wako. Yaani kabla hawajaniteka na kuniua basi video yenu itakuwa hewani”

“U…u…n….a…j…ia…mini nini wewe”

Mrs Sanga alizungumza huku akiwa amejawa na kigugumizi kikali sana. Magreth akaingia kwenye akaunti yake ya google drive alipo hifadhia video hiyo, akaipakua na kumuonyesha mrs Sanga aliye jikuta akizidi kutetemeka kwa woga.

“Hichi ndicho ninacho jiaminia. Sasa wewe nikanyage bahati mbaya mimi nikulipue makusudi. Sitishiki kijinga na wala usipate shida ya kuhangaika kuhisi kwamba nina tembea na mume wako. Ninakudhibitishia kwamba nina tembea na mumeo tena na nina muamrisha vile nipendavyo sasa ngoja nikapandikize sumu ya kukuacha alafu uone kama utaendelea kubaki nyumbani kwake. Mjinga wewe”

Magreth mara baada ya kuzungumza hivyo akaiingiza simu yake ndani ya pochi. Akanyanyuka na kumtazama mrs Sanga anaye kabiribia kupandwa na presha.

“Kamalizane kwanza na kesi yako polisi, au unataka nimuonge RPC akupeleke ndani ukapotelee huko. Eheeee? Nikutakie siku njema”

Magreth mara baada ya kuzungumza maneno hayo, akampa ishara Juma na wakatoka hotelini hapo na kumuacha mrs Sanga akihisi moyo wake ukipasuka kwa presha.

“Vipi bosi mume kubaliana?”

“Mpumbavu yule mama”

Magreth alijibu kwa hasira hukua kifungua mlango wa gari lake na kuingia ndani. Juma akazuguka upande wa pili na kupanda.

“Mpumbavu kivipi?”

“Ananiambia ohoo achana na mume wangu, sijui vimepanda na kushuka. Sasa mimi pale kwenye mgahawa ni wanaume wangapi nina zungumza nao kwa urafiki. Sasa sijui ana nichukuliaje na siku nyingine akija pale kwenye mhahawa. Hakuna kumuhudumia”

“Sawa bosi nime kuelewa”

“Jana mume ingiza kiasi gani?”

“Mulio kumi na moja”

“Moja iache ofisini, hizo kumi chukua gari ukaniletee.”

“Sawa mkuu”

Magreth akafika nyumbani kwake. Akamkabidhi Juma gari lake kisha kish yeye akaingia ndani, Juma akaondoka na kuelekea mgahawani.

“Mbona ume kasirika?”

“Si limke lako lina kuja kunitisha oohoo achana na mume wangu. Nilijua ni mtu wa maana kumbe ananiletea mambo yake ya kifala hapa”

Magreth alifoka hadi nabii Sanga akajawa na mshangao.

“Mke wangu?”

“Ndio kwani na wewe una wake wangapi bwana. Nisikilize kitu kimoja Sanga, japo nina kipenda sana ila maisha ya kuishi kwa vitisho na kutishiwa tishiwa siyataki. Kama una shindwa kumuhimili huyo mke wako niambie kabisa nitafute ustarabu wangu. Umasikini wangu na kupokea hizi mali zako isiwe chanzo cha mimi kuingia kaburini ikiwa hata miaka thelathini sijafikisha. Umenielewa?”

Magreth alizidi kufoka huku machozi yakianza kumwagika usoni mwake. Nabii Sanga akahisi kama kichwa kinalipuka kwa hasira ya gafla aliyo ipata. Hakutarajia kama ipo siku mke wake ana weza kukutana na Magreth.

“Ume muacha wapi?”

“Mpigie bwana mke wako ata kuambia yupo wapi? Alafu unisikilize jambo moja na wewe. Nipo tayari kurudi kwenye kachumba kamoja na kuuza maandazi kwani huo ndio urithi alio niachia mama yangu. Musininyanyase kwa pesa zenu umenielewa”

Nabii Sanga katika kipindi chote hakuwahi kumuona Magreth akiwa katika hali ya hasira kama hiyo. Nabii Sanga akaingia chumbani, akavaa nguo zake haraka haraka, akaichukua bastola yake na kutoka chumbani hapo.

“Kama utashindwa kuachana na mke wako. Tafadhali nina kuomba usirudi hapa nyumbani kwangu tena”

Maneno ya Magreth yakamfanya nabii Sanga kumtazama kwa sekunde kadhaa kisha akatoka nje. Akaelekea kwenye duka la jirani alipo liacha gari lake. Akaitafuta namba ya mke wake na kumpigia, simu ya mrs Sanga ikaita kwa muda na kukatika. Akapiga tena na simu ikakatwa jambo lililozidi kumfanya nabii Sanga kujawa na hasira kali sana.

‘Huyu malaya hanitambui mimi leo ni lazima nimuue kwa maana ana niiingilia sana kwenye raha zangu’

Nabii Sanga alizungumza hukua akiondoka kwa kasi eneo hilo hadi muuza duka akamabaki na mshangao mkubwa.

***

Julieth akafanikiwa kulitoa gari lake polisi, kutokana eneo la mbele limepata itilafu, akamkabidhi mwanasheria wa familia yao kulipitisha gereji huku naye akilitumia gari la mwanasheria huyo kuelekea hotelini alipo Evans. Simu yake ikaanza kuita, akaitoa kwenye mfuko wa suruali yake na kukuta ni mama yake ndio anaye mpigia. Akaipokea na kuweka loud speaker. Julieth akastuka mara baada ya kusikia sauti ya mama yake akilia.

“Mama”

Julieth aliita huku akipunguza mwendo wa gari hilo na kulisimamisha pembeni ya barabara.

“Mama una nini?”

Sauti ya Mrs Sanga ikaka jambo lililo zidi kumfanya Magreth kuchanyikiwa sana kwani hakuwahi kumsikia mama yake akilia kwa uchungu kiasi hicho.

Julieth akakata simu huku machozi yakimlenga lenga, akampigia tena mama yake, simu yake ikaanza kuita na ikakata. Akapiga tena huku jasho likianza kumwagika usoni mwake, simu ikapokelewa na suati ya mwanaume.

“Wewe ni nani uliye pokea simu ya mama yangu?”

Julietha liuliza kwa msisitizo huku akiwa amejawa na wasiwasi mwingi sana.

“Mimii ni msamaria mwema, mama yako amepata ajali hapa Kigamboni na gari lake limedumbukia kwenye mtaro na hapa wasamaria wema tuna jitahidi kumukoa”

“A…a….h…me….pata aj…ali?”

“Ndio na hali yake sio nzuri kabisa”

Julieth akajikuta akiponyokwa na simu yake mkononi. Machozi yakaanza kumbubujika mashavuni mwake na kujikuta akishindwa hata kuendesha gari hilo kwani nguvu zote za mwili zimemuishia.



Julieth taratibu akajipangusa machozi yake. Akaitazama simu yake iliyo aguka pembeni yake. Akaiokota, akaitafuta namba ya mama yake na kumpigia. Majibu ya kuto kupatikana kwa simu ya mama yake yakazidi kumchanganya sana Julieth kwani hatambu ni wapi atakuwepo mamayake.

***

Mrs Sanga akakaa kwa sekunde kadhaa hotelini hapo huku akitafakari aliyo ambiwa na Julieth. Woga ulio changanyika na mawazo mengi sana ukamfanya kichwa chake kuanza kuuma. Taratibu akanyanyuka huku akibebe pochi yake, akaanza kutembea kwa mwendo wa taratibu huku akilini mwake akiwazia video inayo milikiwa na Magreth, endapo ita samba ulimwenguni, basi hato jua ni wapi aiweke sura yake.

“Samahani mama, umesahau kunipatia pesa ya vinywaji”

Muhudumu aliye wahudumia vinywaji alimsimamisha mrs Sanga. Taratibu akafungua pochi yake na kutoa noti ya shilingi elfu kumi na kumpatia muhudumu huyo. Hakujali kuhusiana na chenchi iliyo salia katika kiwango hicho cha pesa. Akatoka nje na kuingia kweye gari lake. Mrs Sanga akaanza kuondoka eneo hilo huku akiliendesha gari lake kwa mwendo wa taratibu sana. Mawazo ya ajali aliyo ipata siku iliyo pita, bado ana yakumbuka vizuri sana. Simu yake ikaanza kuita, akaitazama na kukuta ni simu ya mume wake, mapigo ya moyo yakazidi kumuenda kasi kwa maana ana amini kwa asilimi kubwa, mazungumzo yote aliyo zungumza na Magreth ameweza kuelezwa. Mrs Sanga hakuona haja ya kuweza kuipokea simu hiyo, akakata, ikapigwa kwa mara nyingine, akakata. Hazikupita hata dakika mbili ukaingia ujumbe wa meseji, akaufungua na kuusoma.

‘NIMEKUVUMILIA VYA KUTOSHA SASA LEO NITAKUONYESHA MALAYA WEWE’

Ujumbe huo kutoka kwa nabii Sanga ukamfanya Mrs Sanga kuzidi kuchanganyikiwa, maumivu ya kichwa yakazidi kuongezeka huku yakiambatana na kizunguzungu kikali sana. Mrs Sanga akajikuta akiachia mskani wa gari hilo huku akiishika kichwa chake. Gafla akastukikia gari lake likitoka barabarani na kuingia kwenye mtaro mkubwa ulipo pembezoni mwa barabara hiyo. Gari hilo likaserereka huku mrs Sanga akipiga kelele za kumuta Mungu wake. Gari likagonga kwenye karabati na kusimama. Mrs Sanga akazidi kupandwa na presha, akaichukua simu yake na kumpigia Julieth huku akilia kwa woga mwingi sana. Simu yake ikapokelewa, mrs Sanga akatamani kuzungumza jambo ila kashindwa na kujikuta akilia huku damu zikimwagika usoni mwake, kioo cha mbele kime pasuka. Wasamaria wema wakiwemo waendesha pipikipin a bajaji walio kuwa katika eneo la barabara hiyo wakawahi eneo la tukio. Wakaanza kusaidiana kumtoa mrs Sanga katika gari hilo.

“Huu mama nina mfahamu, ni mke wa nabii Sanga”

Mwenyekiti wa waendesha pikipiki hao alizungumza huku akimtazama mrs Sanga aliye poteza fahamu.

“Tumuwahisheni hospitalini”

Muendesha bajaji mwengine alizungumza.

“Oya hakuna kibaka yoyoye kusogelea gari. Yaani hapa kikiondoka hata kioo cha pembeni ya hili gari tuna dili na vibaka woten na muna tujua kwa maana tuta wasaka”

Mwenyekiti huyo aliuzungumza huku akiwatazama vijana wawili ambao ni wavuta bangi. Mwenyekiti hiyo akainga ndani ya gari hilo, akatoa simu pamoja na pochi ua mrs Sanga. Simu ya mrs Sanga ikaanza kuita, namba hiyo inayo ita ime andikwa my dauther, ikimaanisha ni mtoto wa kike wa mrs Sanga. Akaipokea na kuzungumza na binti huyo. Muendesha taksi mmoja akaileta taksi yake eneo la tukio, wakamuingiza mrs Sanga katika siti ya nyuma, mwenyekiti huyo akaingia hukua kiwaagiza vijana wake kuhakikisha wana imarisha ulinzi katika eneo hilo hadi pale polisi watakapo fika.

“Ila gari ya huyu mama haikuwa kwenye mwendo wa kasi, yaani sijui imekuwaje ame pata ajali?”

Dereva taksi huyo alizungumza huku akiongeza mwendo kasi wa gari lake.

“Ladba kuta kuwa na hali fulani ime mkumba ndani ya gari kwa maana hata mimi nime shuhudia jinsi akidumbukia kwenye mtarao ule”

“Au emelewa?”

“Hapana huyu ni mwana mama nina mfahamu ni mwema sana mume wake ni yule nabii Sanga.”

“Ahaa yule nabii anaye fanya fanya miujiziza ya kuponya watu?”

“Yaa huyo huyo”

“Aisee sasa sijio ame kubwa na nini mama wa watu?”

“Duu simu yake ime zima chaji sasa sijui familia yake tuta wasiliana nayo vipi”

Mwenyekiti huyo anaye julikana kwa jina la Ngoko alizungumza huku akiitazama simu hiyo ya mrs Sanga ambayo alikuwa ana wasiliana na mtoto wa mrs Sanga.

“Duu sasa una uta wasiliana naye vipi?”

“Ninayo namba ya mume wake acha ni mpigie”

“Sawa”

Ngoko akaitafuta namba ya nabii Sanga na kumpigia, simu ikaanza kuita na kumfanya ageuke nyuma na kumtazama mrs Sanga aliyepoteza fahamu.

***

Nabii Sanga mara baada ya kumtumia mke wake meseji ya vitisho, akazidi kuongeza mwendo wa gari lake kuelekea nyumbani kwake. Akiamini kwa asilimia mia moja ata mkuta nyumbani mke wake. Simu yake ikaanza kuita, akaitazama kwa sekunde kadhaa na kukuta ni namba ngeni. Akataka kuikata ila aka ipokea.

“Ndio”

“Habari yako nabii Sanga”

“Salam nani?”

“Nina itwa Ngoko ni miongoni mwa waaumini wa kanisa kalo”

“Una hitaji nini/’

‘Nabi Sanga hapa ninavyo zungumza nina muwahisha mke wako hospitalini. Amepata ajali ya gari na hali yake sio nzuri kabisa.”

Nabii Sanga akafunga breki za gafla za gafla na kuzifanya tairi za nyuma kuserereka barabarani hadi baadhi ya watu walipo eneo hili wakajawa na mshangao mkubwa.

“Amepata ajali wapi huku Kigamboni?”

“Sasa mpelekeni Agakhan niwakut hapo”

“Sawa mchunguji?”

“Nashukuru”

Nabii Sanga akakata simu, kwa haraka akageuza gari lake na kunza kuelekea eneo la hopistali ya Agakhan. Kutokaa na foleni za hapa na pale, ikamchukua nusu saa kufika hospitalini hapo. Ngosha mara abada ya kumuona

nabii Sanga akamfwata na kusalimiana naye.

“Mimi ndio nilite kupigia Nabii”

Ngosha alizungumza kwa unyenyekevu huku akimtazama nabii Sanga.

“Ahaa..shukrani sana ndugu Mungu azidi kukubariki”

“Hii ni simu ya mama pamoja na pochi yake, ni vitu mihimu ambavyo niliona nivitoe kwenye gari”

“Ohoo Mungu akubariki, je hali ya mgonjwa ina endeleaje?”

“Tumewakabidhi madaktari na hadi sasa hivi bado hatujapata jibu. Ila wata kueleza”

Nabii Sanga akaongozana na Ngosha pamoja na muendesha taksi huyo hadi kwenye eneo la chumba anacho fanyiwa matubabu mrs Sanga.

“Nabii nilikuwa nina zungumza na mwanao. Simu ya maam ilikata chaji, hivyo sikumpatia taarifa kamili kwamba ni wapi mama alipo, ila nilifanikiwa kumueleza kwamba mama amaepata ajali”

“Asante sana”

Nabii Sanga akampigia simu Julieth na kumueleza wapo hospitali ya Agakhan na kama ni kufika basi afike haraka sana. Baada ya dakika kumi mlango wa chumba hicho ukafunguliwa na akatoka nesi wa kihindi aliye valia sketi fupi.

“Nesi hali ya mke wangu ina endeleaje?”

“Bado tupo kwenye matibabu, kwa sasa sina la kuzungumza. Samahani”

Nesi huyo baada ya kuzungumza maneno hayo, akaanza kutembea kwa kasi kwenye kordo hiyo na kumuacha nabii Sanga na wezake wakimsindikiza kwa macho tu. Julieth mara baada ya kufika eneo hilo, akaelekezwa na baba yake ni wapi alipo. Julieth akafika eneo hilo na kuwasalimia Ngosha na dereva taksi huyo.

“Mama amepatwa na nini?”

“Kwamaelezo ya hawa vijana walio msaidia ni kwamba amepata ajali. Gari liliingia kwenye mtaro”

“Kwani alikuwa kasi kaka?”

“Hapana alikuwa kwenye mendo wa kawaida sana ambao hatujui ni kitu gani ambacho kilitokea hadi akazama ndani ya mtaro”

“Katika kama hichi hakikisha mama yako huwa aendeshi gari. Ile ajali ya jana nina imani kwmaba bado ina mtafuna akilini mwake.”

“Sawa baba”

“Vijana muna jishuhulisha na nini?”

“Mimi ni dereva pikipiki na huyu mwenzangu ni dereva taksi”

“Kwa kweli nina washukuru sana kwa kila jambo ambalo mume lifanya kwaa mke wangu. Kesho asubuhi nina omba muweze kufika pale kanisani kwangu, kidogo niwapatie kazawadi”

“Tunashukuru sana nabii”

Nabii Sanga akatoa laki mbli na kuwakabidhi.

“Hiyo ni pesa ya mafuta. Ila kesho musikose mida ya saa nne nne kufika ofisini kwangu”

“Tuna shukuru sana nabii”

Ngosha na rafiki yake wakaondoka na kurudi maskani kwao.

“Umefanikiwa kutoa gari lako?”

“Ndio”

“Lipo wapi?”

“Nime mkabidhi mwana sheria alipeleke gereji. Hapa nimekuja na gari lake”

Nabii Sanga na mke wake wakaka eneo hilo kwa zaidi ya lisaa moja na mrs Sanga akatolewa na kupelekwa chumba cha wagonjwa mahututi.

“Dokta ni kitu gani kinacho msumbua mke wangu?”

“Ni mstuko wa moyo ambao tume jitahidi kwa kadri ya uwezo wetu tume hakikisha kwamba hali yake tuna iweka sawa. Je kuna jambo ambalo ni baya lilimpata na kumpelekea kuwa katika wasiwasi?”

“Ndio jana aligonga muendesha pikipiki”

“Basi hakikisheni kwamba muna muweka mbali sana na maswala ya magari na jambo jengine hakikiesheni kwamba hapewi habari za kustukiza, lazima kabla ya kuwepa habari apatiwe muda kidogo ili asipate hilo tatizo la mstuko wa moyo. Mambo mengine tuta endelea kuwaeleza taratibu taratibu”

Daktari huyo wa mwenye asili ya Kihindi aliwaeleza nabii Sanga na Julireth ambao wote wapo kwenye chumba hicho, wakishuhudia jinsi mrs Sanga anavyo hema kwa kutumia mashine maalumu za oksijeni.

“Sawa dokta je kuna tatizo jengine lililo sababishwa na ajali hiyo?”

“Madhara ya ajali ni huko kukatwa na kioo kidogo hapo usoni. Ila hakuna madhara mengine zaidi ya hayo”

“Sawa sawa dokta tuna shukuru”

“Muna dakika tano za kumtazama kisha mutoke”

“Tuna shukuru”

Baada ya daktari huyo kutoka, nabii Sanga akaanza kumuombea mke wake huku wakishirikiana na Julieth. Walipo maliza kusali wakatoka nje ya chumba hicho.

“Kwa nini una msaliti mama yangu?”

Swali la Julieth likamstua sana nabii Sanga kwa maana hakutarajia kulisikia swali kama hilo tena kuto kwa mwanaye wa mwisho ambaye ana mpenda kuliko hata watoto wake wa kwanza wa kiume.

“Nani ame kuambia nina msaliti mama yako?”

Julieth akamtazama baba yake kwa macho ya hasira sana. Machozi yakaanza kumwagika pasipo kulia, ikionyesha ni ishara ya maumivu makali sana ambayo yana toka moyoni mwake.

“Ulishindwa kumuajiri hadi ukaamua kumfungulia Mgahawa tena kwa pesa za familia eheeee?”

Nabii Sanga akazidi kujawa na maswali mfululizo na mshangao, kwani habari hizo anazo zisikia mtoto wake hakupaswa kabisa kuweza kuzifahamu.

“Na…nani nime mfungulia mgahawa?”

“Baba wewe ni mtumishi wa Mungu. Kama una ficha hilo jambo kwa waumini wako, ila tambua Mungu humfichi chochote. Mungu ana ona hadi ndani yako. Angalia baba yangu usije ukamuua mama yangu kwa maradhi. Nina jua kila jambo unalo lifanya na Magreth na hadi jana mama kumgonga yule muendesha pikipiki chanzo ni sisi kufahamu kwamba mupo Bagamoyo hotelini na pale tulikuwa kwenye gari tuna kuja kuwafumania huko. Baba nina mambo yako mengi sana. Tafadhali usi mtese mama yangu”

Nabii akahisi nguvu zikimuishia, taratibu akaka kwenye benchi lililopp nje ya chumba hicho. Julieth akaka huku akijifuta machozi usoni mwake.

“Mama yangu ana pitia kipindi kigumu sana. Anapitia mateso makali sana ambayo hastahili kupitia. Nina imani kwamba hata kuendesha kwake gari taratibu na kulizamisha kwenye mtaro chanzo ni uchafu wako baba kwa nini una kuwa hivyo?”

“Juliy mwanangu”

“Beee?”

“Mama yako yeye ndio ame ifikisha hii familia hapa”

Nabii Sanga alizungumza huku machozi yakimlenga lenga usoni mwake.

“Kivipi ikiwa wewe kiongozi una fanya mambo kama haya. Baba wewe ndio umefikisha hii familia hapa na wala sio mama. Mama alikuwa amesimama asilimia mia moja kwenye dini, ila wewe baba ndio ulimtoa kwenye uwepo huo. Ngoja nikuambie siri ambayo wewe hujui kama mimi nina ijua”

Nabii Sanga akamtazama Julieth kwa mshangao huku akisubiri kuifahamu siri hiyo. Julieth akajipangusa machozi kwa kutumia leso kisha akamtazama baba yake huku macho yakiwa yamejawa na uwekundu utokanao na kulia.

“Mule ndani mimi ndio mtu wa kwanza kugundua kwamba wewe ulifanya mapenzi na yule kijana wa kiume kutoka nchini Nigeria. Baba niliumia sana kwa maana nilisha anza kumpenda yule kijana bila ya wewe kukueleza ukweli. Ila nipo kuona una muingilia kinyume na maumbile, niliumia na kukiri kwamba sinto kuja kukaa na kupenda tena maishani mwangu. Mama alipo shuhudia lile jambo alipoteza hadi fahamu kwa maumivu. Kuanzia pale baba mama hakuwa tayari kukusujudia kwa uchafu ulio ufanya na ndio maana alifanya kile alicho kifanya.”

Maneno ya Julieth yakamfanya nabii Sanga kuanza kutetemeka mwili mzima huku woga ukiwa umemtawala. Siku zote alihisi kwamba siri hiyo ana ifahamu mke wake pekee.

“Hii siri sikuwahi kumueleza mtu yoyote zaidi yako wewe. Sijawaambia kaka zangu kwa sababu sikuhitaji kuisambaratisha familia yangu.Baba”

“Na…anammm”

“Sinto kuja kukaa na kuona familia yangu ina sambaratika kwa ajili ya malaya mmoja ambaye ki umri amenipita sijui ni miaka miwili tu. Yule Magreth unaye tembea naye ni sawa na mwanao baba, hamfikii hata kaka yanu wapili.”

Julieth alizungumza kwa msisitizo huku akilia kwa uchungu mwingi sana.

“Sasa baba ni hivi. Chukua simu yako sasa hivi na umpigie yule malaya Magreth na umueleza kwamba wewe na yeye basii. Usipo fanya hivyo ninaapa kwa Mungu, haki ya Mungu baba nitakwenda kuzitoa siri zako zote kwa kaka zangu na ukiwa mbishi wakuelewa. Nitawaambia waumini wako mauvu yako moja baada ya jengine ambayo umeyafanya ikiwemo kutumia nguvu za giza katika utumishi wako”

Julieth alizungumza huku macho yakiwa yamemtoka kwa hasira, nabii Sanga akahisi moyo wake una pasuka kwa sharti hilo alilo pewa na Julieth, mtoto anaye mpenda kuliko kitu chochote kwenye maisha yake.


“Mpigie simu sasa hivi”

Julieth aliendelea kuzungumza kwa msisitizo huku akimtazama nabii Sanga. Taratibu nabii Sanga akatoa simu yake mfukoni, kabla ya kumpigia simu Magreth, Julieth akampokonya baba yake simu hiyo na kuitafuta namba ya simu ya Magreth, akafanikiwa kuipata. Hakutaka kujishauri mara mbili akampigia huku akiendelea kumtazama baba yake ambaye mapigo ya moyo yana zidi kumuenda kasi sana. Julieth akaishusha simu hiyo kutoka sikioni mwake, mara baada ya kujibiwa simu hiyo haipatikani. Julieth akajaribu kumpigia tena Magreth na kukutana na jibu hilo hilo kwamba namba hiyo anayo ipigia kwa sasa haipatikani hewani. Julieth akaingia upande wa meseji, kwa lengo la kumtumia Magreth meseji kali sana. Ila kabla hajamtumia, akaiona meseji ya baba yake ambayo alimtumia mama yake. Magreth macho yakazidi kumtoka, hasira ikazidi kutawala kifua chake kwani meseji hiyo hakika ni ya udhalilishaji na iliyo jaa vitisho vikali sana.

“Kwa hiyo una muita mama yangu. Malaya si ndio?”

Julieth alizungumza huku akimuonyesha nabii Sanga meseji hiyo. Nabii Sanga akakosa hata nguvu ya kufunua kinywa chake. Julieth akatoa simu yake mfukoni na kutazama muda ambao mama yake alimpigia na kugundua meseji hiyo ilitumwa kwenye simu ya mama yake, dakika tano kabla hajampigia.

“Sio mawazo ya mama yangu ndio yamemfanya apate ajali. Ila ni wewe ndio umesababisha mama yangu kupata ajali kwa meseji ya vitisho hii.”

Julieth aliendelea kuzungumza kwa kufoka huku uso mzima ukiwa umetawaliwa na uwekundu utokanao kwa hasira. Uzuri eneo hilo halina watu wanao pita zaidi ya manesi ambao ni mmoja mmoja sana.

“Julieth mwa…..aa”

“Niache mimi”

Magreth akanyanyuka na kuanza kuondoka huku akiwa na simu ya nabii Sanga. Nabii Sanga akatamani kumfwata kwa nyuma ila miguu yote ime kosa nguvu kabisa ya kumfwata Julieth aliye fura kwa hasira. Julieth akaingia kwenye gari alilo kuja nalo na kuanza kuangua kilio cha uchungu sana. Baba yake amekuwa chanzo kikubwa sana cha mama yake kukubwa na mamatatizo makubwa kiasi hicho.

‘Kwa nini familia yangu ina ingia kwenye shida hizi’

Julieth alizungumza huku akiwa amejawa na hasira kali sana. Akaanza kuikagua simu ya baba yake huku akiendelea kububujikwa na machozi. Akaingia eneo la video, akakuta video mbili tu, akafungua video ya kwanza. Macho yakamtoka huku mapigo ya moyo yakianza kumuenda mbio, video hiyo ina muonyesha mama yake na Tomas wakifanya mapenzi tena ofisini kwa baba yake.

“What’s fuc**”

Julieth alishangaa sana video hiyo. Hakuwahi kumfikiria mama yake ana weza kufanya uchafu kama huyo tena kwenye ofisi ya kanisa.

“Huyu si Tomas?”

Julieth aliendelea kujiuliza maswali hayo. Akazidi kusikiliza mpango wa mama yake na Tomas wa kumteka baba yake. Jambo hilo likazidi kumuweka Julieth njia panda kwani hapo awali alihisi baba yake ndio mbaya kumbe mama mtu ndio mtu mbaya na amefanya vitu vibaya sana ambavyo ni vya aibu hata kuzungumwa kwenye jamii.

***

Hasira kali ambayo ime mtawala Magreth hakuhitaji hata hakuitaji kupatikana hewani. Akazima simu yake na kuingia chumbani kwake na kulala. Kelelee za kengele ya mlangoni, zikamstua na akakurupuka kutoka usingizi, akajifunga tenge na kutoka nje. Akafungua geti na kukutana na Juma.

“Ohoo Juma”

“Samahani nime kusumbua bossi”

“Hapana, japo nilikuwa nime lala. Ehee niambie vipi?”

“Nimekueletea pesa na zipo ndani ya gari.”

“Sawa nashukuru sana”

Juma akaingiza gari hilo ndani, akahesabu kiwango hicho cha pesa na kilipo kamilika, Magreth akatoa milioni moja na kumkabidhi.”

“Kwa ajili ya uaminifu wako”

“Ohoo nashukuru sana bosi”

“Usijali, hakikisha leo mauzo yana kwenda vizuri”

“Sawa mkuu”

“Haya siku njema, uta chukua bajaji hapo nje”

“Nashukuru sana bosi”

Juma akaondoka, Magreth akafunga vizuri geti lake na kurudi chumbani kwake na mfuko wa pesa hizo. Mawazo ya kuondoka kwa Evans nyumbani kwake hapo yakaanza kumtawala kichwani mwake.

“Huyu mjinga ame nifukuzia mwanaume wa maisha yangu. Siwezi kukubaliana na hilo. Nitamfanya jambo baya hadi yeye mwenyewe ata shangaa”

Magreth alizungumza huku akiishika simu yake. Akaiwasha na kujaribu kumtafuta Evans hewani ila hakufanikiwa kuipata simu yake.

“Evans utakuwa wapi mume wangu?”

Magreth alizungumza huku machozi yakimlenga lenga usoni mwake. Siku hiyo haikuwa nzuri kabisa kwake, hakuwa na hamu ya kufanya kitu chochote zaidi ya kulala.

***

“Ngosha”

“Niambie ndugu yangu”

“Nime ifikiria ile biashara ya wasichana nime ona ina lipa sana. Hivyo nipo tayari kuifanya?”

“Kweli kaka?”

“Kwa asilimia mia moja nipo tayari. Jambo la muhimu na kubwa sasa hivi ni kuhakikisha una nipa muongozo mzuri wa nini niweze kufanya.”

“Unajua siko uzri na soko rahisi lipo nchini Tanzania. Kama unavyo jua wadada wa kitanzania jinsi walivyo barikiwa mazaga makubwa na mola. Hivyo huko ndipo kwa kupaangalia kwa jicho la tatu”

“Ila kaka si unajua kwamba Tanzania nina matatizo mengi, itakuwa ni ngumu zana kwa mimi kuifanya hiyo biashara”

“Sawa, kesho kutwa mimi nina kwenda Tanzania, nikirudi nita kupa feedback ya kila jambo. Ila kwa sasa nahitaji kukupa usimamizi wa club yangu”

“Ila kaka hiyo biashara ya Club sija ifanya toka nime zaliwa?”

“Hata mimi sikuwahi kufanya kazi ya Club ila nilifanikiwa kufungua na ikakua na imekubwa ni club kubwa sana hapa Afrika kusini, Hivyo si kila jambo lina hitaji uingie darasani”

“Sawa kaka nime kuelewa”

“Jiandae leo jioni nika kutambulieshe kwa wafanyakazi wangu”

“Sawa sawa”

Jioni ya siku hiyo Tomas akaandaliwa suti nzuri na mke wake kisha wakaondoka nyumbani hapo na kuelekea katika Club inayo imiliki. Tomas akawaita wafanyakazi wote ofisini kwake. Akamtambulisha Tomas na kuwaeleza ata kuwa ndio meneja msimamizi wa shuhuli zote zinazo endelea katika ukumbi huo mkubwa wa starehe. Baada ya utambulisho huo wafanyakazi wakaendelea na kazi zao.

“Unajua lengo la mimi kukuleta hapa uwe una simamia hii biashara uta weza kufahamu ni viwango gani vya wanawake ambao tuta kuwa tuna wahitaji. Pia uta tambua ni aina gani ya unga wenye thamani kubwa na una tumiwa na wataje wetu”

“Sawa sawa kaka”

“Ila kuwa makini usiendekeze ngono, kumbuka hivi sasa una mke”

“Hahaa usijali kaka. Nita hakikisha nina fanya ubunifu mkubwa na hii Club ina zidi kuwa kubwa”

“Sawa ndugu yangu”


ITAENDELEA



0 comments:

Post a Comment

BLOG