Search This Blog

Sunday, May 31, 2020

TRUE VENGEANCE SEHEMU YA 9/10


TRUE VENGEANCE
MTUNZI….EMMANUEL F.KWAY(THE STORY MASTER)
AGE…(18+)
Watchstrap…+255718 862176
SEHEMU YA 9 KATI YA 10
*******
 *******

Muda mchache baadae aliiingia mlinzi mmoja liye valia suti na kumuelezea kuwa kuna
ugeni,alivyoangalia tv yake pembeni alimuona Sesilia akiwa na watu wawili hakukuwa na haja ya kuulizia sababu alijua ugeni huo kutoka Urusi aliwa ruhusu wageni wale na moja kwa moja kuingia ndani,
“Am president Alinga, please have a seat,I hope your mr, Stuwart and Miss Ritah?,(mimi ni raisi Alinga, tafadhali ketini, natumai wewe ni mr, Stuwart na Miss Ritah)”?!
“yes we are the ones,who we were communicating with you in Russia(ndiyo sisi, ambao ulikua una ongea nasi kipindi tupo Urusi).
“its not a big deal, I think I don’t have to say much, your president has already told you the circumstances of my country, I don’t think that you will fail, ”(sio jambo zito, nafikiri sitoongea sana, raisi wenu alishawaeleza tayari maswaibu ya nchi yangu, sitegemei kama mtaniangusha)!.
“with all due respect sir, give us 24 hours , do you have any suspect in custody”(kwa heshima yako kiongozi, tupe masaa ishirini na manne, una mtuhumiwa yoyoyte kizuizini)?”
“am not so sure but I will give you my man to help you out”(sina uhakika kwa hilo lakini nita wapa kijana wangu awa saidie).

Walizidi kuongea mengi ndani ya ofisi ya Raisi Alinga na kupewa uhakika kuwa wange mkamata mtuhumiwa ndani ya masaa machache Stuwart na Ritah walipewa chumba ndani ya ikulu hiyo , jambo lile bado lili kua siri sana,

“HABARI zilizo tufikia hivi punde mbuge Masatu amefariki dunia ghafla usiku wa kuamkia jana..”
Habari ile iliyo kua ikiendelea ili mfanya Witness asitishe chakula anacho kula na kuongeza sauti ya tv na kusogea karibu, moyo ulimuuma sana na kufanya chozi limtoke alicho jilaumu ni kimoja tu, hakuweza kutekeleza kile alicho muhaidi Masatu juu ya kumlinda, kweli alikiri kufanya kosa kubwa sana, hakuelewa afanye nini kwa aliye husika na kifo cha Masatu, ila akili yake ni moja kwa moja ilimtuma ni lazima atakua Mrosso na si vinginevyo,
Hasira zili mkaba kooni kupita kiasi, alicho takiwa hapo ni kufanya kitu kimoja tu kumtafuta Mrosso sababau alijua kivyovyote vile ndiye aliye husika,
Alishuka mpaka chini kwenye andaki lake na kuangalia picha na kuweka duara kwenye picha ya Mrosso, alivyoangalia watu waliobakiza kuwauwa , walikua watu wanne tu amalize kazi yake akiamini akifanya ivyo ataishi kwa amani, ila ki upande Fulani alijua bado ana kazi nzito, mmoja wa watu alio taka kuwauwa ni raisi wa jamhuri ya Muungano Mh, Alinga, huyo ndiye alikua na hasira nae kabisa, na kujua kivyovyote vile ndiye aliye toa agizo kuwa baba yake ndiye auwawe,

Picha za wazazi wake wakiuwawa kinyama bado zili pita kichwani kwake na kuzidi kumtia hasira sana,

Taratibu za mazishi tayari zili kua zime andaliwa kifo kile cha Massatu, kili wagusa sana wana nchi wa Tanzania kila mtu aliumia sababu ya yeye kutaka kusema ukweli kabla ya uamuti kumkuta, walijua fika kuwa kuna njama zime tumika kufanya mauaji ya Masaatu lakini hakukuwa na jinsi ya kufanya,

Mwili uli letwa Dar es saalam kwa ajili ya kufanya taratibu za maziko ya kumpumzisha Mh. Massatu kifo chake kili zidi kuleta gumzo, baada ya kutangaza kuwa alikufa ghafla kwa ugonjwa wa presha,
Magari ya kifaahari tayari yalikua nje ya nyumba yake kubwa na viongozi mbali mbali kuwepo tayari ,
“kaka habari”!
“safi dada, za kwako”?
“nzuri tu, hapa ndo kuna msiba wa Yule kiongozi”?
“ndio dada”
“sasa mbona wewe upo ndani ya gari,”?
“si una jua kazi zetu izi za udereva, mimi siruhusiwi kutoka humu ndani ya gari”
Alikua ni Witnes akiwa na dereva wa Mrosso ndani ya Landcruiser vx mkononi alikua ameshika machungwa mawili moja alikua ana lila na lingine ameshika mkono mwingine
“pole sana, karibu chungwa mi mwenyewe nataka kwanza nipumzike hapa nje baadae niingie”
“asante sana”
Dereva Yule alichukua chungwa lile na kuliweka mdomoni bila kujua lilikua lina dawa kali sana za usingizi, baada ya dakika chache dereva Yule alikua kapoteza fahamu zake na kutulia kwenye kiti,
Alicho fanya Witnes alimvua nguo zake na kumuweka ndani ya Boneti la gari, kisha yeye kuvaa nguo zake na kofia ile ya kipolisi vizuri aki msubiri Mroso aweze kuingia ndani ya gari, hakuelewa ni kifo gani atumie kuumuaa ila alipanga amuuwe vibaya sana, hata ikiwezekana mwili wake usionekane kabisa.

“Bosco, nipeleke lunch kwanza pale pa siku ile”
Kauli hiyo alitoa Mroso baada ya kuingia ndani ya gari. bila kujua aliye kua kwenye usukani ni Witnes kafifi.

 MBELE ya raisi wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Alinga walisimama watu wanne Vincent Towo, Stuwart ,Ritah na mshauri wake Mbetto peke yao ndani ya ofisi yake,alionekana kabisa ni kama mtu aliye changanyikiwa sana, bado marafiki zake wa karibu walizidi kuuwawa kikatili alitambua fika kuwa sasa kifo chake kina karibia, Alisha ihamisha familia yake kwenda uingereza kimnya kimnya akiamini huko watakua salama salmin , aliinua kichwa juu ya meza na kuwa tazama watu waliosimama mbele yake kama milingoti , kisha akawaruhusu kila mmoja akae kwenye kiti,
“Towo sio kwamba sija pendezeshwa na kazi yako, usiji sikie vibaya, huyo unae muona hapo ana itwa Stuwart na huyo ni mwenzake ana anaitwa Ritah, wame tokea nchini Urusi, naomba muungane muwe kitu kimoja, ili tuweze kumu weka huyu muuwaji kizuizini,”
Alizidi kuongea Raisi huku wote wakiwa wametega masikio yao ili kusikia vizuri kile kilicho kua kina zungumzwa,

“sawa muheshimiwa Raisi, kama nilivyo kwambia hapo Awali kuwa nita kuhakikishia kuwa nita mtia mikononi huyu muuaji, nili fanikiwa kutoroka kwake kama ni ivyo sitoshindwa kumtia nguvuni, nakuhakikishia kuwa nitafanya nao kazi hawa bega kwa bega”
Mambo aliyokua ana ongea Vincent Towo yalikua hayana ukweli kabisa ukweli ni kwamba alikua ana mjua muuaji, alibeba siri nzito sana ndani ya moyo wake, alijua kuwa Raisi wake sio mtu mzuri kabisa aliamua kwa moyo wote aweze kumsaidia Witness ambae wazazi wake waliuwawa kinyama sana,
Aliwa tazama wageni wale na kuwapa mikono huku akitabasamu ,
Ivyo ndivyo ilivyo kua .

LAND CRUISER vx lilizidi kusonga mbele wakati huo bado hakujua kuwa aliye kua ndani ya usukani ni Witnes kafifi, aliji tanua nyuma upande wa kushoto na kuweka tai yake vizuri,, hakujua kuwa kifo chake kipo jikoni kwa wakati huo,laiti ange lijua hilo ange fungua mlango na kutoka kasi ya ajabu,
“sasa tukirudi uta nipitisha kwenye ile gest kama kawaida sawa”
Bado aliongea mwenyeawe akidhani kuwa aliye kua mbele ni dereva wake, ila cha kushangaza aliona milango ina jifunga kwa LOCK , alivyoangalia kioo cha mbele cha kati kati aliiona sura nyingine tofauti kabisa huku gari hilo likizidi kuongeza mwendo kasi kabisa,
“wewe nani”?
“kaa kimnya”
Aliongea Witnes akionyesha hasira za wazi wazi kabisa, alitoa bastola na kuiweka juu ya dash bod na kuingia barabara ya ukonga, gari lilizidi kunyooka mwishowe kufikia katika kimsitu kidogo na kumuomba Mroso ashuke nje, hakutaka kuongea mengi alimtandika risasi ya paja na kumfanya apige kelele nyingi sana, alimpiga risasi nyingine ya mguu wa kushoto na kumpakia ndani ya gari, huko alizidi kupeleka gari mbele kisha akalipaki pembeni ,
“najua ndani ya kichwa chako una jua kwanini haya yanatokea”!
“naomba usiniue!”
“siwezi kukusamehe hata kidogo naenda kukuuaa, tena ngoja nikwambie jinsi nita kavyo kuua, hili bomu naenda kuliweka ndani ya gari ufie humu”
Kweli alilokua akiongea alikua akimaanisha sana sababu alishika bomu mkononi na kuliweka ndani ya gari ambapo alianza kumfunga Mroso na kamba ngumu za manira ndani ya gari. Kisha kutoka nje baada ya hapo alitembea umbali mdogo na kutoa rimoti ambayo ilikua na antenna ndefu,
pale pale alibonyeza kitufe chekundu na kilicho tokea hapo ulikua ni mlipuko mkubwa uliosikika kwa nguvu sana, na kufanya hata kunguru na ndege wa angani kuruka huku na kule,

*****

“have you heard that(umesikia hiyo)?”

Ilisikika sauti ya Stuwart ndani ya chumba kidogo cha C.I.D (central investigation criminals) headqutal wakiwa katika kikao cha mwisho ambacho kilikua sasa na wapelelezi wengine wanne, bomu lile hakika lilisikika katika kila pembe ya kona na kufanya hata hofu kuingia kwa wana nchi wa kawaida,
“yeah what is that?(ndio kwani nini hiko).”
Alihoji Ritah ndani ya chumba hiko wote walikua kimnya kabisa, kupitia redio upepo waliweza kujua kuwa kuna mlipuko wa bomu haraka haraka ili wabidi wawashe magari yao na safari ya kwenda ukonga kuanza Vincent akiwa juu ya usukani huku kushoto kwake akiwa Ritah na nyuma kushoto alikaa Stuwart wote walikua wamenyonga tai zao kama wakurugenzi.
“Ritah nikwambie kitu”
Alizungumza Stuwart wa lugha la kirusi ili Vincent asielewe.
“niambie stuwart”
“nina mashaka na huyu jamaaa”
“kwanini unasema ivyo”?
“navyo mwangalia ana onekana ni mtu mwenye mashaka mashaka sana, sina imani nae”
“niambie cha kufanya”
“fanya juu chini upate simu yake, uweke kile kinasa sauti nataka nijue watu wote atakao zungumza nao na kifaa cha kutafsiri sauti, maana tangu nime kuja namuona muda wote yupo walu walu, nime soma saikolojia, kuna kitu kichwani mwake”
“sawa hakuna tabu”
Gari zilizidi kuchanja mbuga Vincent akiwa ana ongoza msafara huku nyuma yake kukiwa na magari mawili gari zote zilikua MARK X nyeusi , ziliwasha taa na kutoka kasi za ajabu, kupitia redio upepo waliweza kufika eneo la tukio ambapo waliona tayari magari ya polisi yalikua yame tanda huku pembeni yake kukiwa na raia wakizunguka na kushangaa tukio hilo la kushangaza.
Gari zile zilipiga misele na wote kushuka haraka haraka,
“Mr, Towo may i have your phone please(Mr, Towo naweza nikapata simu yako tafadhali)?!
“no problem”!(hakuna tatizo)
Towo alitoa simu yake mfukoni na kumkabidhi Ritah kisha yeye kushuka na kuvaa koti jeusi la suti huku akiongozana na Stuwart nyuma yake, walitoa vitambulisho na kupita ndani ya uzio mwekundu ambao ulikua umewekwa,
Walichokiona ndani ya gari ulikua ni mwili uliioungua vibaya sana na kuonekana fuvu kabisa, picha zilishaanza kuchukuliwa na mapolisi ili uchunguzi uweze kufanyika, ila pale pale Stuwart aliomba copy ya picha zile na kuzidi kulichunguza gari lile, alivyo litazama kwa ujuzi wake alijua kabisa ni aiina gani ya bomu lililofumua gari hilo,

Bado akili yake ilizidi kucheza juu ya nini afanye sasa ili aweze kuingia ndani ya nyumba ya waziri mkuu ambayo ilikua na kila aina ya ulinzi kila kona aliwaza sana, alitaka kuyafanya mambo yake haraka haraka sana , ili aweze kuka milisha mauaji yake, hakua na jisni zaidi ya kumtafuta Towo kwa njia ya simu,
“ndugu, tuna weza kuongea sasa hivi”?
“subiri kidogo sipo sehemu nzuri…….enhe tunaweza kuongea sasa”!
“sitaki kuongea kwenye simu ni maongezi marefu sana”
“sasa ina kuaje,”?
“una pajua kwangu”?
“ha ha ha ha ndio napajua,”
“sawa sikia sasa njoo usiku saa tatu, njoo peke yako”
“poa ntakuja”
Yalikua ni maongezi baina ya Towo na Witnes kupitia simu ya mkononi,
Hakuelewa ata mpata vipi waziri mkuu ili amuuwe na kisha amtafute Raisi Alinga bado kazi ilikua ni ngumu kwake kama kumuuwa kubwa la maadui, sababu watu hao walikua na ulinzi wa kutosha kila pembe, ila kitu kimoja katika maisha yake alikua mtu asiye kubali kukata tamaa.
“ina bidi nimalize kile nilichoanza”
Aliwaza Witnes huku akiwa jikoni ana pika chakula cha usiku ili pia Towo aje kula nae pindi ataka po kuja, baada ya chakula kile kuiva aliingia kwenye friji na kuchukua juice kisha kutenga mezani na kuanza kula huku akizidi kutafakari mambo mengi sana, alimuwaza sana Austine mpenzi wake ambaye alikua

nje ya nchi na kumuhaidi kuwa akirudi waweze kufunga ndoa kisha wajenge familia, alitaka kabla ya ndoa awe keshamaliza kila kitu chake,awe kesha wauwa wabaya wake, na kulipiza kisasi,

Baadae usiku kufika Towo alifika na kufunguliwa geti na mlinzi na kuingia ndani, baada ya salamu Witnes hakusita kumuelezea shida yake aliamini Towo wana muamini sana serikalini ivyo kupitia yeye ataweza kumvujishia baadhi ya siri kutoka huko,
“nikushauri kitu?”
Alizungumza Towo huku akimtizama Witnes machoni mwake,
Na kumfanya Witness akae vizuri na kutega sikio lake vizuri alitingisha kichwa kuashiria kuwa Towo aanze kumshauri
“kesho kutwa kuna mchina tuna msafirisha kwenda BEIJING ila mimi sitoenda, nita kua kwenye huo msafara, huko kwao china alikua ana kesi ya kunyongwa akatoroka Hongkong, akapanda meli mpaka Afrika kusini, akitumia hati feki, sasa huko china alikua na tuhuma za kuji badilisha sura na kuiba wakati mwingine kuua, akaja na mitambo yake huku, baadae wakamgundua, serikali ika muomba wampeleke huko kwao, ili akanyongwe, jamaa anaitwa shu gang Lee , sasa hiyo ni historia yake fupi, huyoo mchina atakusaidia kukubadili sura kila kitu, ukitaka hata sura ya nani”
Habari zile zili mfanya mpaka Witnes atabasamu, kwa upande wake hakuwai hata siku moja kuwaza kubadili sura yake pengine aliona wazo hilo ni bora kuliko mengine yote aliyowahi kufikiria.
“enhee”!
“sasa basi kesho kutwa saa kumi jioni, fanya juu chini utuvamie ili umteke huyo mchina, ukisha mteka mimi nita kwambia cha kufanya , najua kazi hiyo ni ndogo kwako”
“ha ha ha ha ha ha ha, nita fanya iyo kazi, “
“mimi nita kupa ishara”
Mazungumzo hayo baada ya kuisha Towo aliaga baada ya kula hapo na kuondoka zake huku nyuma akiwaza ni jinsi gani ataweza kumkamata muuaji huyo.
MARK Xnyeusi mbili zilikua mbele katika mwendo wa kasi huku nyuma yake kukiwa na gari la magereza ndani yake alikua mchina aliye itwa shu gang Lee akiwa na pingu mkononi na miguuni kote, alionekana dhahiri kuwa ni jambazi sugu pembeni yake kulikua na maaskari walioshika mitutu wakiimarisha ulinzi wa hali ya juu,
Nyuma ya magari hayo kulikua kuna mapiki piki meupe na defender nyingine tatu hakika ulikua ni ulinzi wa kuji dhatiti,

“nikimaliza kazi yangu, utaendelea na safari yako”!
Alizungumza Witness akiwa na bastola mkononi akimuweka dereva wa gari lile chini ya ulinzi, huku akiwa juu ya usukani wa gari kubwa aina ya Scania iliyokua na mzigo wa mafuta, alipiga gia na kuzidi kupandisha gia kwa mbali sana aliona magari ya mapolisi na kuhama upande wa juu walikua tayari wamefika TAZARA maataa ambapo walisubiri taa za kijanani ziwake ndipo safari ianze, taa zili waka na Witnes kupiga gia, alizidisha kasi mpaka kukaa sambamba na gari hilo la magereza ambapo ndani yake alikuwepo Mchina,
Bila kupoteza muda alikunja usukani na kuligonga gari la magereza na kulifanya lipoteze uelekeo na kuhama kabisa barabarani

 Taaraifa za redio upepo zili fika mpaka makao makuu CID(central investigation department). Walilala mika kuwa wame vamiwa ivyo wame zidiwa na wanahitaji msada wa haraka, Stuwart akiwa kwenye

kikao hiko akiwa elekeza njia za kumkamata muuaji huyo ili mbi-di asitishe zoezi hilo na kuongozana na jeshi hilo dogo .walitoka nje na kutafuta gari ndogo na safari ya kuelekea eneo la tukio kuanza ,a lichukua bastola yake na kuiweka sawa sawia na kumtizama Ritah,
“are you ready for this(upo tayari kwa hili”)?
“yes”

Stuwart alirudisha shingo upande wa pili huku dereva wa gari hilo akiwasha king’ora kuwa kuna dharura , ndani ya dakika kadhaa tayari walifika eneo la tukio na kuwaona baadhi ya maaskari wamesimama nyuma ya milango yao

wame jificha huku milango ya magari yao ikiwa wazi, lakini cha ajabu hakuna hata mmoja aliyeweza kurusha risasi, mbele yake aliona roli la mafuta na gari la magereza likiwa chini lime pinduka,
“nini kinaendelea”?
Alihoji stuwart akitumia lugha ya kiingereza
“mpaka sasa hivi sija jua ila mkuu ame tuambia tusipige risasi”!
“nani huyo”?
“Towo”
“yuko wapi”?
“yupo kule upande wa pili”
Stuwart kimnya kimnya alipita huku akiwa ame inama na kumuendea Towo ambae alikua uponde wa pili, bila kupteza muda ili bidi amuulize kisa cha yeye kukataza askari kupiga risasi.
“kuna gari la mafuta, nime toa kauli moja risasi zisirushwe”
“hapana, tuta mkosa mtuhumiwa”
“nisikilize mimi nipo incharge”
“am not taking orders from you, am taking orders from your president,”(sichukui amri kutoka kwako nachukua amri kutoka kwa raisi wako”
Alijibu stuwart huku akikoki bastola yake na kuzidi kusonga mbele.

Witnes akiwa ndani ya gari la magereza ame muweka mchina mfungwa chini ya Ulinzi alizidi kutafakari sana. Kwa kuwa walisha panga njama na Towo jinsi ya kutoka, bila kujua Stuwart teyari kesha ingia,
Risasi zilianza kusikika na kumfanya Wity aanze nayeye kujibu mashambulizi yale akirusha nayeye risasi upande walio simama maaskari.

Risasi zilianza kurushwa sasa baada ya kupewa kauli kutoka kwa Stuwart akiwa mwenye hasira sana alivua koti lake kisha kuji ficha kwenye moja ya gari huku akichungulia upande wa adui una orusha risasi, kwa ishara ya mkono alimwambia Towo apite upande wa pili bila kujua hakua upande wake sasa.
“Witnes sikia, pita hivi tafuta gari hawa niachie mimi!”
Alizungumza Towo baada ya kumfikia WITNES KAFIFI
“na huyu mchina”?
“ondoka nae sisi tuta wasiliana, fanya haraka”
Witnes alitoka haraka haraka upande wa pili, kwa mbali sana Stuwat aliweza kumuona kupitia mgongo wake na kuiweka bastola yake jichoni akimpima kwa jicho moja Witnes eneo la mgongoni,

Towo alivyo geuka aliiiona hali ile hakua na la kufanya zaidi ya kupiga risasi lori la mafuta na kusababisha mlipuko mkubwa sana, Stuwart alirushwa upande wa pili huku baadhi ya mapolisi kila mmoja kutupwa upande wake,
Kitendo kile Ritah alikiona alimfuata moja kwa moja Towo na kuipiga teke bastola yake kisha kukunja ngumi na kuanza kupigana pale pale, Towo alirusha teke ila kwa utaalamu wa hali ya juu Ritah aliinama na kumbeba na kumbwaga chini, kitendo cha kusababisha mlipuko utokee ulijibu kabisa swali lake kua ana wasaliti, alitoa taarifa moja kwa moja kwa Stuwat na kufika eneo lile akiwa anavuja damu puani,
“where is she,”?(yuko wapi”?)
“I don’t know(sijui)”
“you gonna tell me on one way or other(utaenda kuniambia kwa njia moja au nyingine)
Aliongea Stuwart na kumpiga kichwa puani Towo kwa nguvu na kuanza kumshambulia ngumi nyingi hususani maeneo ya usoni na tumboni, licha ya kupigwa kiasi kile lakini hakuwa tayari kufungua kinywa chake kuzungumza ukweli, ilikua ni bora afe, mafunzo ya kutotoa siri kizembe yote alikua nayo ivyo kumtesa vile ilikua ni kazi bure,

Askari tayari walimzunguka na kuja ribu kumtoa lakini wote walishindwa na baadhi yao kupigwa vilivyo, hakua yeye tena hasira zili mtawala ndani kwa ndani,alizidi kushusha kipondo mpaka Towo alipozirai. Bila kujua muuaji alikua ni mpenzi wake Witness ambaye aliyempenda kwa dhati na kudhani ame kufa.
“Ritah Take him to custody, four biyometric package, I need him to tell me the truth, from today I will be incharge, do you understand me,(ritha mpeleke chumba cha mahojiano, pakiti nne za biyometric, nataka aniambie ukweli, kuanzia leo mimi ntakua kiongozi,mmenielewa)”.
Pale pale ilibidi achukue simu ya kiganjani na kumpigia Raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania mheshimiwa

Alinga na kumueleza mambo yaliyotokea, habari zile zilii msikitisha sana hakuelewa kwanini Towo ana mgeuka , ila hakua na jinsi zaidi ya kuku bali Stuwart awe kiongozi na kumhakikishia ata mpa kila kitu pale ata kapo kwama,
baadhi ya wapelelezi wali chukizwa lakini hawa kua na jinsi zaidi ya kukubali uongozi ulioendeshwa na Stuwaty ambae muda wote alionesha dharau au pengine ni mchapakazi kuliko mtu mwingine,
Towo alibebwa na kuingizwa ndani ya gari kisha safari ya kurudi makao makuu CID kuanza , waliingia ndani na kumfungia ndani ya chumba maalumu kwa ajili ya mahojiano,

“Stuwart scottlah the director of CID, I know who you are, stop screwing up, so when was your first time to met her?help me to understand the side of yuour story Mr, Towo fair enough I don’t wanna torture you,because if you wont cooperate , I will and am sure you gona tell me”
(stuwart scottlah mkurugenzi wa CID, najua wewe ni nani, usicheze na mimi, kwaio lini ilikua mara ya kwanza kuonana nae? Nisaidie kujua historia yako Mr, Towo , ki haki sitaki kukutesa, sababu usipo toa ushirikiano, nita fanya ivyo na nina uhakika uta nieleza”

Alizungumza Stuwart akiwa ndani ya chumba hiko cha mahojiano ambapo kilikua maalumu kwa watuhumiwa baada ya kusema ukweli ndipo upelekwa mikononi mwa sheria ili hukumu itoke,
Upande wa Vincent Towo mpaka dakika hiyo hakua tayari kufungua midomo yake kusema lolote lile, katika kichwa chake aliamini kuwa Witness hana hatia yoyote ile, ivyo kumtaja alipo ili maanisha kutokumaliza mambo ana yotaka kufanya.
Kidude kidogo kama kiredio kili letwa na kuwekwa mezani kisha kuwashwa kili cho sikika hapo yalikua ni maongezi ya

Vincent Towo na mwana mke ambaye yeye aliiitambua sauti ile ilikua ni ya Witness kafifi,
Ritha alileta mtambo mwingine mdogo wa kubadili lugha kisha baadae kujua kile kilichokua kina zungumzwa, walishika namba zile na kuingiza kwenye mtambo mwingine ambao uliweza kuwaonesha simu ya mwana mke huyo ilipo, mambo yalifanyika dakika mbili na kujua wapi Witnes alipo,
Waliweka scrin kubwa kupitia mtambo wa GPRS waliweza kujua kila kitu, haraka haraka gari zilikuja na jeshi dogo kuanza safari ya kuelekea MSASANI usiku huo huo tena bila kupoteza muda huku waki muacha Towo ndani ya chumba kile kidogo .

*****

BAADA YA kufanya kitendo cha kuteka nyara na kumuweka Mchina Yule kama mateka katika nyumba yake jingine ambayo haikumaliziwa bado iliyopo chanika yeye alirudi na kuingia nyumbani kwake kwa lengo moja tu kuchukua kila kitu na kuhama eneo hilo ili aweze kubadili sura,
alishafanya uchunguzi wake siku hiyo hiyo na kupata sura ya msichana wa ndani wa kazi aitwaye Debora ambaye alifanya kazi nyumbani kwa waziri mkuu, alitaka ajibadili sura yake na kuwa kama Debora aliamini kabisa kufanya vile inge kua rahisi kumuua waziri mkuu sababu ange kua karibu nae sana , alipanga panga mabegi yake, na kuweka nguo

zake huku mkononi akiwa na picha ya Debora ambae kidogo miili yao ili endana japo sio sana,!
Ila kabla ajamaliza kitu alihisi miungurumo ya magari ikiwa nje alivyo chungulia nje aliona geti lime pigwa teke kisha watu kuingia wakiwa na bastola zao mikononi, alivuta begi lake haraka haraka, ,na kwenda mpaka kwenye main switch ya umeme na kuizima, kitendo kile kili fanya kiza nene kutokea sababu aliizoea nyumba yake haikumpa shida, alianza kumfyatua risasi mmoja baada ya mwingine,aliye kua akiingia mlangoni. Alivaa begi mgongoni na kutoka mbio mlangoni risasi nyingi zikimkosa kosa, aliinama chini chini zikiwa zina piga ukuta huku akikimbia.
Ila kabla ya kutoka nje alihisi maumivu makali juu ya bega lake na risasi kupenya mkononi na kumfanya adondoke chini kifudi fudi.
“its over your under arrest(yame kwisha, upo chini ya ulinzi).
Hakua na chaguo lingine akiwa chini huku mkono wake ukiwa umelowa damu nyingi na kuhisi maumivu makali sana , ilisikika sauti iyo na kutulia pale pale alipo.
 Taratibu aliingiza mkono wake mfukoni na kutoa kitu kama kiazi mfukoni ambacho kilikua na kipini juu yake, kwa kutumia mdomo taratibu alitoa pini ile ya bomu aina ya grinade kisha kulitupa nyuma ya mwanamke Yule.

“GRENADE”!

Ritah aliropoka na kilicho fuata hapo ni kila askari kusambaratika akitafuta usawa wa kuokoa maisha yake, sababu walijua nini maana ya msemo ule wa bomu ilo ambalo likitolewa kipini una tokea mlipuko wa ajabu, wote walijitupa chini na mlipuko ule kutokea na kusababisha moshi mweusi mkali sana,
kufumba na kufumbua hawa kumuona Witnes kwa mbali walisikia muungurumo wa gari ukitokomea waaliishia kulikimbiza kwa miguu na kupiga risasi lakini walikua teyari wamesha chelewa sababu Range aliyo kua akitumia ilikua mbali tayari ikiishia kukata kona, huku wakiishia kuona taa nyekundu kwa nyuma.
“mme mkosa”?
“ndio Stuwart”
“shiiit, tumfuate Towo atakua ana jua kila kitu, GPRS vipi”?
“simu yaake ameiacha humu ndani ime ungua”
“fuc*****”!

Alitukana Stuwart huku akiyabana meno yake kwa hasira, baada ya kumkosa muuaji ambaye tayari walikua wana karibia kumuweka mikononi mwao!, mawazo ya kumfuata Towo yalimjia kichwani na hasira kumbana kwa lengo moja tu, amtese sana mpaka atakapo sema ukweli, juu ya mwana mke Yule ambaye mpaka wakati huo hakubahatika kumuona sura yake.

****

RANGE ROVER spot nyeusi lilizidi kuchanja mbuga likitoa mwendo wa kasi sana kuliko kawaida , ndani yake juu ya usukani alikuwepo Witness kafifi, akiendesha gari na mkono mmoja huku mkono mwingine ukiwa una vuja damu nyingi, alichukua matambala na kuingiza mkono ule uliokua una vuja damu ili kuzuia damu isitoke nyingi, alihisi maumivu makali sana ndani ya mkono wake wa kushoto, alivua tishirt yake na kubaki na sidiria kisha kuingiza kidole chake ndani ya jeraha.
“aaaaaaaaah”!
Alipiga kelele za maumivu, zoezi alilotaka kulifanya halikufanikiwa sababu risasi ilikua mbali sana, alikimbiza gari mpaka alivyofika chanika, na kulificha gari ndani ya
kimsitu kidogo kisha kufungua mlango, alitoa mabegi yake na kushuka akielekea kwenye mjumba huo ambapo alimkuta mchina shu gang Lee akiwa na pingu mkononi ambapo alikua amefungwa pembeni ya chuma,
Alipita na kulala juu ya meza kubwa kisha kufungua begi lake, alichukua kibiriti na kutoa njiti moja kisha kukwangua chenga chenga za kibiriti kile,kisha kumimina kwenye jeraha la risasi,
“Nidhungulie nisaidie wewe”!
Aliongea mchina huyo kwa Kiswahili chake kibovu.
Witnes alimtizama na kushika bastola yake na kumuwekea.
“kaa kimnya”!
“mimi taka saidia wewe, kufanya ivyo si dhawa, naweza saidia wewe, ukapona kabidha kabidha”!
“unanijua mimi nafikiri, uki fanya upumbavu wowote ule nitakuua”
Witness alisimama na kutoa funguo kisha kufunga pingu alizokua amefungwa kisha kurudi juu ya meza na kulala, moja kwa moja mchina Yule alimuendea Witnes na kuanza kukagua kidonda chake kisha kutumbukiza kidole chake ndani ya jeraha lile,
Matitabu ya haraka haraka yalianza pale pale huku mchina yule akiji tolea kumsaidia kabisa Witness aliamini kabisa sio mtu mbaya kwake sababu tangu amteke hakuwahi kumfanyia ubaya wowote ule,
Baada ya risasi ile kutolewa alitoka nje na baadae kurudi na majani kisha kuyafunga pamoja na bandeji, ndani ya siku kadhaa tayari hali ya Witness ilikua vizuri ya kuridhisha , alimshukuru sana Mchina Yule na kumuelezea kisa cha yeye kumteka nyara.,
Alimuonesha picha ya Debora kisha mchina Yule kucheka na kumwambia kuwa ni kazi ndogo ila hapo alipo hana mitambo,
Waliwasha gari na kuelekea K,koo usiku sana wa siku iyo na kuingia mpaka kwake na kuchukua mitambo hiyo, waliipakia ndani ya gari kisha kurudi mpaka Chanika, walijenga tayari urafiki kwa muda wa siku chache ,
Witnes alidungwa sindano ya usingizi na kulala nusu kaputi, na kufanya mchina Yule aendelee na kibarua chake alimchoma sindano nyingine ya kupunguza mwili kidogo, kila alilo lifanya alilifanya kiumakini akitumia picha aliyopewa na Witness, baada ya masaa mawili kila kitu kili kua sawa na Witnes kusimama,
Alikiendea kioo hakuamini alivyo jiangalia kwenye kioo aliona sura ya Debora vile vile kuanzia juu mpaka chini, alibaki akimtizama Shu gang Lee kwa mshangao mkubwa!.
“ipo safi hiyo, bado kitu moja, sauti ya huyu musichana nataka fanya iwe kama ya kwake”
“hakuna tabu ninayo”
Witnes aliiingia kwenye begi na kutoa kinasa sauti alicho mrekodia kisha kumpatia, mchina Yule aliingia kwenye

mtambo mdogo na kuweka kompyuta yake , kisha kuingiza sauti ile kwenye mashine nyingine na kukiweka kitu kidogo kama kidonge, baada ya nusu saa aligeuka na kumwambia ameze kidonge kile.
Alichukua maji na kumeza kidonge kile kweli sauti yake kabisa ilikua kama ya Debora na kuamini kuwa China sio nchi ya mchezo, kweli hata ukimwangalia usingeweza kumjua kua ni Witness, alibana nywele zake kwa nyuma kama Debora na sasa kua kama mwana mke huyo.
“kazi yangu ita kua nyepesi sasa”!.
Aliwaza Witnes huku akikitizama kioo cha mbele yake.

*******

MATESO MAKALI YALIZIDI kwa Towo akiteswa sana kwa wiki nzima na Stuwart kila aina ya mateso ili afungue kinywa chake aseme ukweli, lakini haikuwa ivyo haikuwa rahisi kama Stuwart alivyo dhani hapo awali, licha ya kuteswa sana lakini hakuthubutu kusema ukweli wowote ule,
ilkua bora afe kuliko kumsaliti Witness kafifi ambae alijua huko alipo ana lipa kisasi cha wazazi wake waliokufa miaka mingi iliyopita na aliyesababisha mauaji hayo ni chama kilicho kua madarakani.
“una jipo..teeezea mu..da wako. Ha ha ha ha ha ha ha. Niu..e tu mpumba…vu ha ha ha ha”
Aliiongea Towo akiwa na damu nyingi mwilini alililia sana kwa maumivu aliyo pata lakini hakua tayari kusema lolote, alicheka kicheko cha dharau na kumtemea mate yaliyo changanyika na damu Stuwart aliyekua akimpiga mbele yake, kipondo cha mbwa mwizi kilizidi kuendelea sana akizidi kupigwa ngumi na kuchapwa mikanda, alichomwa mpaka na pasi yenye moto mgongoni lakini hakua tayari kutoa siri,
Mafunzo ya kipelelezi aliyo funzwa ya kuto kutoa siri kizembe, ndiyo ulikua muda wake wa mtihani wakati huo,!

Ritah alimuita Stuwart nje na kuonekana dhahiri kua kuna jambo ana taka kumueleza.
“plan A ime shindikana , sasa tutumie plan B”
“una maana gani”?
“ana familia huyu, mke na watoto wawili, ana mke wake yupo sehemu moja iitwayo Zanzibar, bububu kitu kama hiko”!
“basi nisha kuelewa fanya mipango hiyo, leo hii familia yake iwe hapa, atasema tu”
Wazo hilo lili muingia sana Stuwart akilini , taratibu za kutafuta familia ya Vincent Towo ilianza mara moja na baadhi ya maaskari kuteuliwa kupanda ndege na kwenda kuchukua familia yake Zanzibar. ,

haikuchukua muda sana tayari mke wake aliye itwa Neema Towo, na watoto wake wawili wadogo Rachel na Govvan, walikua makao makuu C.I.D . hawa kuelewa kwanini waliletwa ghafla eneo lile,
Walikaribishwa wakae kwenye viti kisha kuhojiwa baadhi ya maswali na Stuwart, waliyajibu kama ipasavyo kisha Stuwart kurudi mpaka ndani ya chumba alichokua Vincent akiwa amelowa damu mwili mzima na kuchakaa kabisa!.
“Una mke mzuri, una watoto wazuri sana Rachel na Govvan!.,”
“una semaje?, naomba usiusishe familia yangu, “
“wewe ndo uli taka tufike huko, mimi sikupenda kufika huko kabisa”
“Ritah”!
Stuwart aliita kwa hasira akimuita Ritah kisha, Neema na watoto wadogo wawili kuletwa mbele yake, mke wake

aliangua kilio alivyo muona mume wake yupo katika hali ile, wote walilia hawa kuelewa nini kime tokea.
“ongea na mumeo vizuri, kuna kitu tuna taka kujua, dakika tano nawapa”
Aliiongea Stuwart na kutoka nje huku nyuma yake akiacha vilio vya uchungu.
“what are you gonna do(utaenda kuwafanya nini)”?
“just wait and see(subiri utaona).
Walisemezana Stuwart na Ritah, baada ya dakika tano aliingia ndani ya chumba hiko na kukaa pembeni ya Vincent na Neema huku nyuma yake walisimama watoto wawili wadogo wakiwa wanalia.
“nafikiri muda ume watosha”!
“hata uni fanye nini sito sema”
Pale pale Stuwart bila huruma kama umeme alichomoa bastola yake kiunoni na kuifyatua mguuni mwa Neema.

“talk to me, son of a bitch”!

Aliropoka Stuwart kwa hasira na kumpiga tena risasi Neema ya mguu wa pili na kumfanya adondoke kifudi fudi chini huku damu ziki mvuja sana,
kili kua ni kitendo cha kinyama sana na kufanya askari waingie ndani lakini wote walitulizwa baada ya kuwekewa silaha ile.

“back off, stay away from this, I have orders from your president.(rudini huko, kaeni mbali na hili, nina amri kutoka kwa raisi wenu).!

Aliongea Stuwart kwa hasira na kufanya sura yake ijikunje usoni.
Towo alilia kama mtoto mdogo akiwa amekaa juu ya kiti kitendo cha kumuona mke wake kapigwa risasi huku wanae wakilia sana, alitamani kuchomoka kwenye kiti lakini alishindwa kutoka sababu ya pingu alizofungwa, alihisi uchungu sana .

“kacha kacha”!

Aliikoki bastola yake tena kisha kuweka usawa wa mtoto mdogo Rachel kupitia macho yake amabayo tayari yalibadilika rangi kulikua kuna kila aina ya dalili kua hakua katika hali ya mchezo,
alikua kweli na nia ya kufyatua risasi mtoto Yule Rachel ambae alikua akilia sana huku akiwa juu ya mwili wa mama yake mzazi.
“Basi nata..ja nataja….. nata…ja muuaji sasa.. hi..vi yupo. Kwa waziri mkuu”
“ana uhusiano gani na SHU gang Leee?”
“ana ana ana taka kuji badili su…ra ili amuuwe waziri mkuu. Alimtaka kumtumia huyo Mchina afanye kazi yake”
“waziri mkuu ana wa fanyakazi sabini na tatu, ana taka.. kuji badili sura ya nani?”
“haki a Mungu hapo sij..ui hakuniambia”
“unanitania, haitoshi . paaaaaaaaa”
Ilipigwa risasi nyingine na kupenya mkononi mwa Neema na kufanya ukelele uzidi ndani ya chumba hiko.
 BADO WALIMUONA Towo ni muongo hataki kuongea kitu waliendelea kumtesa Neema mke wake ambaye alikua hana hatia hata kidogo, ki ukweli hakustaili kuusishwa kwenye swala lile,Stuwart hakua na utu hata kidogo alizidi kumtesa pia na kumdunga Towo sindano za dawa ya byometric ambapo dawa hio ikiingia mwilini ina kufanya utetemeke kama
mtu aliye kuwa ana pigwa shoti ya umeme au mwenye kifafa, aliona haitoshi na sasa aliweka vidole vya Towo mezani na kuchukua kisu kikubwa kwa nia moja tu akate kidole kimoja baada ya kingine,
amri hiyo aliipokea kutoka kwa Raisi Alinga, kuwa apige hata ikiwezekana amuuwe kabisa na kumpoteza duniani, ili mradi amtaje muuaji ambaye kwa sasa alikua na machungu nae, amri hiyo kwake aliiona ndiyo fursa pekee ya kumtesa bina damu mwenzake tena bila huruma ,
isitoshe mbele ya Neema pamoja na watoto wake wawili wadogo Govvan na Rachel, muda wote walikua wakilia machozi wakimuonea huruma sana baba yao,
Japokua walikua wadogo lakini walijua ni kiasi gani baba yao kipenzi na mama yao ana teseka juu ya kiti alicho fungwa.
“nita endelea kukutesa mpaka uhai wako utakapo kwisha, ngoja nikwambie kitu kimoja, utafia hapo hapo juu ya kiti, na kushuhudia mke wako ana vuja damu na kufia pale pale chini huku una ona”
Aliongea maneno ya kejeli Stuwart..baadhi ya wapelelezi waliokua wana shuhudia waliona kabisa kitendo kile ni cha kinyama wakibaki tu kumlaumu Raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania ndani ya mioyo yao kwa kutoa kauli hiyo bila kufikiria mara mbili mbili. Hata Ritah pia Alisha ingiwa na huruma na

kumuinua Neema mwanamke mwenzake aliye kua chini ana vuja damu mwilini huku akilia kwa maumivu makali, ilikua ni picha ya kusikitisha sana. Machoni mwake.
“Ritah, sio kazi yako muache huyo mwanamke hapo alipo”
“hapana Stuwart sio kiivyo”!
“ni amri, nimekwambia muache hapo hapo”
Alifoka Stuwart huku akipiga meza kwa hasira na kumfanya Ritah arudi nyuma alielewa sana hasira za Stuwart ivyo alihofia maisha yake.
“griii griiiiii”
Simu ilisikika na kila mtu kumtizama Vincent Towo sababu simu hiyo ilisikika kutokea ndani ya mfuko wake wa suruali, Stuwart alisogea karibu na kuitoa kisha kuitazama ilikua ni namba ngeni.
“ndiyo yeye”?
“si….jui”
“Ritah, naomba trace hii simu leta hilo begi”
Haraka haraka Ritah alisogea na begi dogo kisha kulifungua na kuiweka ile simu ndani ya kifaa maalumu na kuichomeka kwenye kifaa chenye mitambo, na baadae kuweka kinasa sauti kina chobadili lugha yoyote ile, walifanya mambo yote yale haraka haraka na kumwambia Towo apokee simu yake,
“you say anything I don’t like it, she dies, UNDERSTOOD?. Karakacha,!”(ukisema chochote kisicho nipendesha , atakufa, nimeeleweka?. )”
Alizungumza Stuwart huku akiweka bastola yake ndogo kwenye utosi wa Neema, kweli simu ile aliipokea Towo na sauti ya mwana mke kusikika upande wa pili.
“Towo uko wapi, nakusibiri wewe”
“mimi nipo nii….po ofi,si,,ni”
“mbona una ongea ivyo una shida gani”?
“haaaaaapana sina shi..da yoyote ile nambie,”
“laki…tititi”
Simu ile ili katwa ghafla na kufanya Stuwart ashindwe kuelewa nini kime fanya simu ile ikatike.

*******

Baada ya kuona kimnya sana Witness aliamua kuta futa simu ambayo alipewa na shu gang Lee aitumie kwa wakati huo, baada ya kumtafuta Towo na kuongea nae mchina Yule alimpora ile simu na kuikata.
“kwanini ume kata hio simu wewe”?
“wana sikiliza sisi hawa, naona hapa kwa mitambo yangu, si dhawa kabisa, wana jaribu kujua wapi tulipo,”
Aliongea Shu gang Lee huku akiuendea mtambo wake na kumuonesha jinsi walivyo kua wakiingiliwa kwenye mitambo yao, mchina huyo kweli alikua ni jambazi mwenye mitambo mingi sana, .
“lazima kutakua kuna tatizo, wame mkamata Towo , lazima nifanye kitu, lazima niende kumuokoa, nita muhitaji kwenye kazi zangu, “

Aliwaza Witness huku akiwa ameweka mkono kwenye shavu lake. Pale pale alisimama na kutafuta kinyago huku akianza kupakia silaha ndani ya begi lake kubwa hakutaka kumuacha Towo alijua ni lazima atatoa siri licha ya hayo alijua atakua ni msaada pekee kwake yeye.
Shu gang Lee hakua na sababu ya kumuacha Witness aende peke yake nayeye alimuunga mkono na kuanza kuandaa silaha za kutosha na mabomu, baada ya kila kitu kwenda sawa walibeba mabegi yao migongoni na kuingia ndani ya Range usiku huo na kutoa mbio, walifika kariakoo na kuchukua piki piki kubwa aina ya BMW ,
Shu gang Lee alipakia na kuvuta mafuta na kufanya lipige kelele nyingi sana.
“shika vizuri kiuno yangu”!
Aliongea Mchina na Witness kutii, piki piki ile kubwa sana yenye bomba mbili ilichomoka kwa mwendo wa kasi sana, wote wakiwa juu ya pikipiki hiyo wakiwa wamevalia nguo nyeusi sana huku wakiwa na maelement vichwani mwao walikua na wazo moja tu , kuvamia MAKAO MAKUU usalama wa taifa kitengo cha CID na kuharibu ofisi izo kisha kumuokoa Vincent Towo.

Shu gang Lee alizidi kukoleza mwendo kasi na kufanya piki piki hiyo itoke mbio mithili ya risasi iliyo toka ndani ya chemba ya bastola. Walisha fika karibu sasa, na kuliona geti na kumuomba Witnes amshikilie kwa nguvu zake zote, baada ya kulikaribia geti lile ki utaalamu sana alinyanyua tairi la mbele la piki piki hilo na kulishusha juu ya geti na kulifanya lidondoke chini,
alizidi kupenya ndani , kabla ya kufika mwisho walisikia milio ya risasi zikirushwa upande waliopo, kila mtu aliji gawa kivyake na kuingilia mlango wake,

Witnes alivaa kinyago na kutoa bastola ambapo aliweka kiwamba kina chozuia sauti ya bastola kutoka, alipita kimnya kimnya na kuwa piga risasi za miguu watu alio waona mbele yake na kusonga mbele.
“Towo yuko wapi. Nijibu fasta”!
Aliongea kwa Ukali Witnes huku akimuwekea mtu mmoja bastola ya utosi.
“yupo yupo, we nyoosha moja kwa moja, kona ya kushoto mlango wa kwanza”
Baada ya kutoa maelezo hayo alipigwa na kitako cha bastola kichwani na kudondoka chini chali.
Alitembea na kuingia ndani ya chumba alichokua Towo huku bastola yake akiwa ameitanguliza mbele, Alisha muona Towo amelala kwenye kiti huku akivujwa na damu,
Ila katika hali ya kushangaza bastola yake ili pigwa teke na mwanamke aliye kua nyuma ya mlango,a livyo rusha ngumi Witness aliiidaka na kumpiga kichwa cha puani na kumfanya mwana mke Yule alirudi nyuma kidogo na kukaa sawa,

alikunja ngumi na kukaa vizuri kwa mpambano na mwana mke mwezake, alimtizama kidogo na kuliona teke lina lokuja usawa wa kicwani na kuweka mkono wake kiufundi.
teke hilo lilidunda na kutupa ngumi ambayo ilipita hewani baada ya mwana mke Yule kuinama kidogo na kupokea ngumi mbili za haraka haraka tumboni,
Witnes alianza kupigana sasa akiwa makiin sababu alijua kuwa mwanamke anaye pigana nae alikua ana uwezo sana wa kupigana kwa jinsi alivyomuona mapigo yake, huku Witnes na Ritah wakiendelea kupigana ,
Chumba cha pili Shu gang Lee alikua akirusha mateke ya hewani akipambana na commando Stuwart akitupia mapigo ya kong fuu, Stuwart alimsogelea na kumkaba kohoni ila Alijikuta yupo chini baada ya
mchina Yule kujilegeza na kumkata mtama kwa chini, baada ya kuinukaa alipokea mateke mawili ya kifua aina ya air kick na kumfanya Stuwart aende chini, aliokota bastola iliyo kua chini ila pale pale ilipigwa teke na kudondoka chini.
“uwaaaaaaaaaa”!

Mchina huyo alipiga kelele izo na kukanyaga meza kisha kujizungusha na kumtandika Stuwart mateke mengine yaliyotua kifuani na kumdondosha chini mzima mzima, alitoka chumba kile na kumfuata Witnes na kuanza sasa kumshambulia Ritah na kumpiga vilivyo, walimfungua Towo na kumbeba wakiizungusha
mikono yake mabegani mwao.
“Neema, na f..amilia yangu”
Towo alijitoa kwao na kuanza kutafuta familia yake aliwa kuta wame fungiwa kwenye chumba kingine kidogo wote walisaidiana na kuchukua funguo za gari kisha kuweka bomu kubwa ndani ya chumba hiko,

Na kutoka nje mbio mbio, walimuingiza Neema na watoto wake ndani ya gari kisha kuvuta antenna ya rimoti hiyo ili kulipua bomu walilotega, kabla ya kufanya ivyo ilisikika milio ya risasi nyuma yao ikipasua vioo vya gari lao walilokua wamekaa ndani na baadhi ya vioo kuwadondokea Neema na watoto wake,
huku wapelezli wakija sehemu waliyokuwepo, Towo alikaa sawa pamoja na mchina Yule na kuendelea kufanya mashambulizi.
Witnes alibonyeza kitufe cha bomu hilo ambalo lilitegwa dakika tano kurudi nyuma, ila cha kushangaza
baada ya bomu hilo kuwaka huku dakika zikirudi nyuma gari walilo kuwemo ndani lili goma kuwaka.
“come on”!
Aliropoka Witnes huku akiangaika kuwasha gari hilo , sasa dakika zilizidi kurudi nyuma na mwishowe kubaki dakika mbili ili bomu lili puke na kuwa uwa wote, maaskari walizidi kuwa fikia walipo huku waki rushia risasi zao. Na kuwa fanya wazidi kuchanganyikiwa.


 Hatimae ilibaki dakika moja tu bomu lile livyatuke kisha mlipuko huo utokee na ikiwezekana waliokua karibu wachanwe chanwe, bado risasi zilirushwa na waliokua ndani ya gari Govvan na Rachel pamoja na Neema waliambiwa walale chini ya viti, huku wakiwa wameinamisha vichwa vyao, na hapo ndipo gari

liliwaka. haraka haraka Witnes aliweka gia na kutoa kasi ya ajabu baada ya sekunde chache walishaanza kusikia milipuko nyuma yao, na kufanya jengo hilo la CID kuteketea moto, walitembea umbali kidogo usiku huo huku ukimnya ukitawala. Hakuna aliye weza kuongea, siti za Nyuma Witnes alisikia kama kwikwi la mtu akilia .alivyogeuza shingo yake alimuona Towo akilia huku akiwa amemkombatia mke wake Neema ambapo dalili zilionesha kabisa kuwa tayari ameshapoteza maisha kutokana na risasi nyingine ya kifua aliyo pigwa, pale pale Witnes aliweka mguu kati na gari kusimama ghafla alishuka na kuhakikisha kama ni kweli aliyo yaona,
Rachel na Govvan walilia machozi, alichofanya Witnes aliwachukua na kumuomba Lee atoke nao pembeni, Towo alilia sana huku akiwa mwenye hasira.
“Towo,pole sana”
Aliongea Witness huku akimshika bega Towo ambaye alikua akitokwa na machozi kuondokewa na mke wake duniani, alimtizama Witnes kwa hasira kali sana.
“pole ya nini na yote uliyataka wewe, bila wewe yote haya yasingetokea,umeiingiza familia yangu kwenye matatizo, wacha nirudi kwa Yule mwanaharamu”
Aliongea Towo kwa hasira huku akiyabana meno na kumsukumiza Wity pembeni ila alitulizwa, kwa hasira alirusha ngumi ila Witnes aliidaka na kumuweka vizuri pembeni ya gari akiwa ame mkaba kooni.
“Nisikilize Towo, baba yangu alikatwa kichwa nimeshuhudia kwa macho yangu, mama yangu mzazi alibakwa na zaidi ya watu kumi nilivumilia, tazama sasa ivi nilipo, mfano ninge chukulia hasira unadhani ingekuaje, wewe ni mwanaume, ina kubidi utumie akili, bado unasafari ndefu sana, pungzua hasira hazitakusaidia”
Alizungumza Witnes kwa sauti iliyo jaa uchungu ilikua ni kama ana kumbuka matukio ya kikatili aliyo fanyiwa hapo nyuma yake, ili bidi Towo atulie na kupunguza jazba zake sababu hakua na la kufanya Neema alisha fariki tayari,japo kua ilikua ni vigumu kuamini kile alichokiona, alitamani japo arudishe siku nyuma ili angalau amuage kwa mara ya mwisho.
walipanga mikakati ya kuingia nyumba ya waziri mkuu huku baadae wakifanya taratibu za kumzika Neema kimnya kimnya bila kujua mtu yoyote Yule, sasa hivi nayeye Alisha fuata taratibu za ukomando, hasira na chuki alizokua nazo Towo ndani ya nafsi yake hakika hazikuelezeka,
alipanga kwa mikono yake kumuuwa Stuwart,mtu aliye mpenda duniani Alisha kufa tayari sasa alibakia na watoto wake wawili ambao alitakiwa kuwalinda ipasavyo.
Rachel na Govvan walichukuliwa na kufichwa mbali sana wakiamini kuwa huko wata kua salama kabisa,siri hiyo walibaki nayo Towo na Witness.
“usimpigie simu mtu yoyote Yule sawa”
“sawa”
Walikua wakiongea huku wakielekea katika nyumba ya waziri mkuu ndani ya gari huku mchina Yule akiwa anaendesha , walifika hapo na kuegesha gari nje, Towo Alisha wahi kufanya kazi ndani ya nyumba hiyo kubwa, ivyo alikua anajua namba zote za CCTV kamera alimtajia mchina Yule na baada ya dakika chache walikua wakiona kila kitu kinachoendelea ndani.
“Yule dada huyo hapo, sasa utafanya njia gani atoke nje mimi niingie?”
“nina namba za simu ya mezani ya chumbani kwake”
Alisema Towo kisha namba ile kupigwa, walimuona akitembea mpaka kwenye meza na kupokea ile simu.
“embu njoo unipokee mizigo yangu hapa nje ya geti”
“sawa nakuja”
Tayari Debora alianza safari ya kutoka nje akijua ameongea na mtoto wa bosi wake.

*****

0 comments:

Post a Comment

BLOG