Search This Blog

Sunday, May 31, 2020

BEDROOM PROFESSIONALS SEHEMU YA 10 MWISHO



BEDROOM PROFESSIONALS
MTUNZI….EMMANUEL F.KWAY(THE STORY MASTER)
AGE…(18+)
WatsApp…+255718 862176
SEHEMU YA 10 KATI YA 10 MWISHO
*******


Marietha Deo Karekezi,ama mke halali wa Deo Karekezi.Akawa kama mtu aliyechanganyikiwa na
maisha,kwanza hakuamini kama alipona baada ya Mzee Maximo kumpitishia risasi pembeni ya masikio yake kisa tu aligundua siri nzito ya kuwa wanaye,Abraham na Wiliam waliuwawa na mzee huyu,jambo ambalo bado hakutaka kukubali, kuliamini hata kidogo.

Siku zote alikuwa ni mtu wa kulia kila kukicha,machozi mpaka yakamkauka lakini hilo halikuweza kubadilika hata kidogo,alihisi kujuta mpaka basi.
Mzee Maximo,hakuwa tayari kumpoteza Marietha,aliamini kwa jambo la kuwauwa watoto wake lingefanya aishi naye kwa raha mustarehe, lakini mambo yakageuka kwani Marietha alijuwa kwamba yeye ndiye mkandarasi wa kila kitu kutokea,alivyomkumbuka mumewe Deo Karekezi, ndiyo akalia na kusaga meno,kumbukumbu ya yeye kwenda na kumtia kituo cha polisi, ndiyo ilimuumiza zaidi,wakati mwingine alitamani aende jikoni na kujitoboa na kisu afe, ama mambo yote yageuke na kuwa ndoto,ashtuke!Kufumba na kufumbua kila kitu kikawa kimeharibika,watoto wake wamekufa wote.
“Abraham… Wiliam…Abraham Wiliam…”
Siku tatu baadaye,akawa anataja majina ya watoto wake!Hakula, wala kufanya kitu chochote kile,akawa kama mtu aliyerukwa na akili kabisa,kila apoongeleshwa na Mzee Maximo, yeye alitamka majina mawili tu,hali hiyo iliendelea mfululizo kwa miezi kumi.Maximo,akajaribu kumvumilia kwa muda wa mwaka mmoja lakini wapi!
“Siwezi kuishi na chizi.Chinga,mwite na Ndanda.Njoeni hapa kwangu leo,”akakata simu na kupiga fundo moja la pombe kali iliyokuwa kwenye glasi. Siku hiyo akawaita watu wake wa kazi,kuna jambo alitaka kuwaeleza.Walivyofika,wakaingia mpaka seblen,wakapeana mikono na tajiri yao kisha kuketi,vitini!
“Nimewaita hapa,kuna jambo nataka mlifanye chapchap”
“Sawa mkuu”
“Huyu mwanamke ninayeishi naye hapa.Amerukwa na akili,nataka mkamtupe mbali sana”
“Wapi bosi?Tupo tayari”
“Nishapata wazo,nitakuwa sio muungwana.Mtupeni nyumbani kwao kule maduda sijui madule.Nadhani Chinga,unapafahamu”
“Ndio”
“Kazi hiyo ianze usiku,mtamuweka pale getini bila mtu yoyote kujua”
“Sawa”
Kikao hiko cha dakika tano,kilivyoisha wote wakatawanyika.
Ilivyofika jioni,vijana wa kazi wakaingia ndani ya jumba hilo,ambapo Maximo alikuwa akiwasubiri.Marietha,alikuwa chumbani,analia tu.Kazi yake ilikuwa ni kutaja majina ya watoto wake!
“William Abraaham..Abraham Wiliam”
Marietha,alisema hayo maneno huku akiwa anashangaa shangaa kama msukule, aliyefufuka.Hakutofautishwa na maiti sababu haja zote alizitoa humohumo ndani ya nguo zake,akawa ana toa harufu kali kama, yai viza!
Usiku wa saa nne ulivyofika,wazee wa kazi wakaingia chumbani,wakamfunga kamba za miguuni na mikononi,wakamuingizia matambala mdomoni kisha wakambeba na kutoka naye nje,huko walimuingiza ndani ya gari na safari ya kwenda maduda kuanza mara moja!
Marietha,alikuwa viti vya nyuma,mikono yake na miguu vimefungwa kamba,vioo vyeusi sana yaani tinted,hakuna mtu yoyote aliyejuwa kinachoendelea ndani ya gari.
Watu hawa hawakutofautishwa na wahalifu, wanaosafirisha magendo kwani jambo hilo lilikuwa siri kubwa sana,safari ilianza mara moja,usiku huo huo.
Lakini cha ajabu walivyokata kilomita kumi na mbili,mbele walikumbana na tochi nyingi,walivyoangalia vizuri wakaogopa kwani mbele kulikuwa na diffenda na askari wamesimama barabarani,wanapiga doria.
“Askari!”
Dereva,akasema kwa hofu.
“Sasa itakuwaje?”
“Mimi sijui lakini fanya unavyojua tupite hapo.Msala mkubwa huu”
Dereva wa gari,akashusha gia baada ya kuona,amepigwa mkono ili aweke gari kando,hofu ilizidi kuwatanda baada ya askari kuanza kusogea karibu na gari,akiwa na tochi pamoja na mtutu begani.
“Aroo,washeni taa za ndani kwanza.Tuwaone”
Kuwasha taa za ndani,kulimaanisha operesheni yao kufikia tamati kwani wangeonekana na Marietha angeonwa,akiwa amefungwa kamba!


Ilikuwa ni katikati ya usiku, mzito sana!Na magari yalikuwa ni machache kupita eneo hilo,kutokana na matukio ya ujambazi ilifanya usiku na mchana maaskari wawe makini sana kukagua magari kwa ajili ya usalama,amri hiyo ilitoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,ndiyo maana askari walifanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha kuwa hali ya amani inarudi kama hapo awali,hivyo ilikuwa kila gari ikipita ni lazima likaguliwe kwa staili ya kuhoji watu waliokuwa ndani ya magari ikifuatiwa na ukaguzi wa hali ya juu,magari yalipekuliwa sio mchezo, viti vilibinuliwa.Askari walikuwa wana usongo kutokana na wenzao kuuwawa huko Kibiti,hiyo ikafanya wapandishe mori na kupandwa morali.
“Aroo nimesema washeni taa za gari”
Askari huyu mkurya alikuwa mwenye usongo na alizungumza kwa hasira huku akichomoa bastola yake kutoka kiunoni,gari aina ya Verossa yenye vioo vikali vyeusi iliyokuwa mbele yake, ilimfanya aanze kupatwa na mashaka,kitendo cha taa kuchelewa kuwashwa ikafanya aweke bastola yake kwa tahadhari na kujihami,huku nyuma maaskari wengine wakiwa makini na tochi kali pamoja na mitutu,mabegani.
Sio siri,dereva wa gari hilo aliyefahamika kwa jina la bwana Gada Abuu,akahisi kutetemeka, kuonekana kwa Marietha kungezua maswali mengi na wangehusishwa moja kwa moja na kesi ya utekaji nyara,mawazo yake yalimtuma apige gia na kukanyaga mafuta mengi,lakini alivyoshika Gia, Chinga akamshika mkono!
“Unataka kufanya nini?”
Chinga akamuuliza bwana Gada.
“Kutimua,msala huu”
“Tulia,acha mapepe kaa kimya,niachie mimi nimalize”
Chinga,alizungumza kwa kujiamini na hakuonesha kuwa na wasiwasi wa aina yoyote ile,ndiyo maana akadiriki kuwasha taa ya ndani,askari wote wakasogea karibu na gari.
“Ko!koo!koo!”
Askari mmoja akagonga kioo,na kuwapa ishara kwamba washushe kioo cha gari,Chinga akafanya hivyo bila hofu,hiyo iliwashangaza sana wenzake!
“Za kazi afande?Naona mpo kazini”
“Ndio,mnaerekea wapi.Usiku huu?”
“Hapo mbele”
“Ebwana,nimekuuriza mnaerekea wapi?Mbere ndio nini?”
“Hospitali,tuna mgonjwa”
Chinga,alivyosema hivyo akageuza shingo nyuma.Tochi ikapigwa ndani,Marietha akaonekana akiwa amefungwa kamba!Ukimya wa kama sekunde tatu ukatokea!
“Aroo,mtoe huyo Mama kitambaa.Nyie ndio watekaji nyie.Mnampereka wapi?”
Tambala alilowekewa Marietha mdomoni,likatolewa!Askari walitaka kuhakikisha ni mgonjwa ama mateka,ndiyo maana wakasubiri,kumsikiliza mwanamke huyo azungumze kitu lakini cha ajabu alikuwa akitaja ‘Abraham,William,Abraham,William’
“Jina rako nani?”
“Abraham,William.Abraham William”
Marietha alizungumza huku akimwaga machozi,ki ukweli akili yake ilikuwa tayari imeharibika, kutokana na vifo vya watoto wake,maaskari hawakutaka kuridhika na jambo hilo.
“Anaumwa nini?”
“Sisi tumeagizwa tu”
“Na nani?”
“Mumewe”
“Yeye Mumewe yuko wapi?”
“Ngoja nimpigie simu”
“Kwanza shukeni ndani ya gari”
Hicho ndicho kilichotokea,kila mtu akateremshwa,msako wa ajabu ukatokea.Maelezo waliyotoa watu hawa,yalifanya maaskari wawawekee mashaka, ndiyo maana hata buti la nyuma likafunguliwa, tochi ikapigwa ndani.
“Halloo Boss,tumekamatwa hapa.Ndio na maaskari…ndio ndio huyu hapa…zungumza naye”
Chinga,alivyotoa simu sikioni baada ya kuongea na Tycoon Mutumbuka Maximo, tajiri aliyewatuma wakamuweke Marietha nyumbani kwao Maduda,akamkabidhi askari.
“Ongea naye”
Askari,akaweka simu sikioni.
“Jambo afande?”
Maximo akaanza mazungumzo.
“Nani wewe?”
“Mutumbuka Maximo”
Askari,alivyosikia hivyo akatoa simu sikioni na kuangalia namba!Jina la tajiri huyo lilimtisha kidogo kwani aliishia kumsikia na kumuona kwenye luninga,akarudisha tena simu sikioni!
“Aroo,Mutumbuka yupi?”
“Kuna vijana wangu,mmewazuia.Mke wangu ana hali mbaya,naomba uwaachie vijana wapite”
“Sawa mzee,inabidi kidogo wakaguliwe.Ni protocol za Kazi”
“Basi wacha nimpigie IGP Mabena ili mzungumze vizuri”
Afande Abbas Marwa alivyosikia habari za IGP Mabena,akahisi kama amepungua uzito ghafla,kupigiwa simu moja kwa moja kwa mkuu wake wa kazi tena na tajiri kama Maximo,ilimaanisha kibarua chake kuota nyasi.Ndiyo maana akapata kigugumizi cha ghafla na simu ilivyokatwa tu,akatoa ruksa!
“Mama pole sana,ebu muwahishe shemeji hospitari.Fanyeni haraka aroo”
Askari,akasema.Vijana wakapiga gia na safari ikaanza tena!
Safari iliwachukuwa kama dakika sitini na mbili nzima, ndipo walipofika maduda na kitendo cha kuwasiri tu,walizima taa za gari na kuanza kumteremsha Marietha kimya kimya huku mdomo wake ukiwa umefungwa,mikono na miguu vimezungushiwa kamba ngumu,wakamuweka nje ya geti na kurudi ndani ya magari yao,wakageuza na kuondoka zao!

****** *****
Ilikuwa kidogo Mama Grace apige ukunga,baada ya kutoka nje asubuhi sana na kuona jambo ambalo lilimshtua nje ya geti lake!Mwanamke aliyelazwa chini,alifanya arudi haraka na kuwaita ndugu zake wengine.
“Kuna nini?”
“Njoeni muone”
“Mama Grace, kuna nini lakini?”
Mama Grace,hakuelewa aseme nini, lakini alitaka ndugu zake watoke nje ili baadaye waende kituo cha polisi kwenda kutoa taarifa za tukio hilo la mtu kuwekwa nje ya geti lao,walivyotoka nje,wakaonekana kupigwa na butwaa la waziwazi.
“Jamani,huyu Mama hajafa kweli?”
Vaileth,akamgeukia Mama Grace na kumuuliza.Kitendo cha kushauriana, wakaona mwili uliokuwa chini,unajitingisha kila mtu akaogopa na kupiga hatua kumi nyuma,Mama Grace ndiyo kabisa,akaingia ndani ya geti na kujifungia, akiwaacha ndugu zake nje, wanagonga geti.
“Fungua geti, Mama Grace”
Vaileth,aligonga gonga geti huku anatizama mwili uliokuwa chini,moyo wake ukapiga kwa nguvu baada ya kuona sura aliyoifananisha ingawa hakuwa mwenye uhakika,akatulia kidogo ili kufananisha sura ya Marietha na Mwanamke mchafu, anayetoa harufu mbaya aliyekuwa chini kafungwa kamba kila mahali.
“Mama Grace,ebu fungua”
Geti likafunguliwa,Mama Grace akatoa shingo!Kiwiliwili kipo ndani,Mama huyu alikuwa muoga kuliko kawaida.
“Sasa unaogopa nini?Marietha huyu”
Vaileth,akasema tena kwa kujiamini, akasogea mpaka karibu na mwili uliokuwa chini,kitu alichokiona kilimuogopesha mwenyewe,ni kweli alikuwa sahihi, Marietha ndiye alikuwa chini,anatoa harufu kali, nywele zake chafu zina vumbi,wakamsogelea karibu zaidi!
“Mariethaaa!!”
Vaileth,akaita kwa uchungu.Bado hakuelewa ni kitu gani kilimpata Marietha,akashangaa ajabu!Hapo hapo wakazunguka na kuzifungua kamba za miguu na mikono,wakalitoa tambala lililokuwa mdomoni mwake.
“Marietha,Mariethaa”
Wakamuita kwa staili ya kumtingisha, mithili ya mtu anayeamshwa kutoka katika usingizi mzito,lakini badala yake Marietha, alianza kutaja majina ya watoto wake.
“Abraham na Wililam wamefanya nini?”
Wakamuuliza kwa pamoja.
“Abraaaham,wiliam”
Hizo ndizo sentensi mbili alizokuwa, anazungumza mwanamke huyu,hata walivyomchukuwa na kumuingiza ndani, ilikuwa hivyo hivyo,walichofanya ni kuingia naye bafuni,wakamuogesha na kumvalisha nguo safi.Hawakutaka kupoteza wakati,wakampigia simu Maximo ili kumpasha kilichotokea,lakini jibu walilopata, liliwafanya wabaki njia panda.
“Mungu wangu!Kwangu,aliondoka muda kidogo.Sikujua alipoenda”
Maximo akajibu kitu cha uwongo!Tena,akionesha mshtuko wa waziwazi simuni.
“Leo tumemkuta getini hapa,amefungwa kamba,ana kitambaa mdomoni”
“Unasemaaaa?”
“Ndio hivyo shemeji,ebu njoo tujue tunafanya nini”
“Sawa,nitakuja”
Ili Maximo kuuwa soo! Na kuwapumbaza, akafunga safari siku hiyohiyo na msafara wake mpaka Maduda,alivyomuona Marietha, akajifanya ameumia kupita kiasi,akakamua machozi mililita saba pointi mbili ili kusindikizia uwongo wake,ilikuwa kidogo Bwana Chinga aachie kicheko sababu hakuwahi kujua kama Bosi wake ni msanii namna hiyo.
“Marietha mkeee wangu.Ulikuwa wapi?”
Maximo,akamvuta Marietha karibu na kumkumbatia akijifanya ana uchungu,Mama Grace na Vaileth,wakajisikia kumuonea sana huruma.Wakamtoa!
“Nitahakikisha nitamjua aliyefanya hivi.Haki ya Mungu tena”
Maximo akaongea kwa hasira,akaingiza mkono mfukoni na kutoa kiasi cha shilingi milioni mbili,akitaka Marietha apelekwe hospitali mara moja,jambo hilo ndilo likawapumbaza kabisa,hakuna hata mtu mmoja kati yao, aliyeweza kuhisi kwamba Maximo ndiye mkandarasi wa kila kitu kutokea.
Baada ya hapo mzee huyu akaondoka!
*********
Kuanzia siku inayofuata,wakawa kiguu na njia wakizunguka hospitali zote ili Marietha apatiwe matibabu lakini wapi,kila walipojaribu kumtibu ikashindikana.Wiki moja ikakatika,Mwezi ukapita,hatimaye mwaka lakini ugonjwa wa Marietha ukawa palepale.Kilichowashangaza zaidi ni baada ya Maximo,kuwafungia vioo.Akawa hapigi tena simu kutaka kujuwa hali ya Marietha na wakimpigia hapokei na akipokea ni lazima angetoa majibu, yasiyoeleweka.
“Nimeshawaambia mimi nipo bize,tafadhali msinipigie simu”
Siku hiyo Maximo,akaongea kwa kufoka simuni.
“Lakini shemeji,Marietha anaumwa”
“Mimi dokta?”
“Pesa za matumizi”
“Sina”
“Dokta amesema,ile mirija ni shilingi laki tatu kubadilisha.Alafu chakula chake kimeisha”
“Nimesema sina,mwache afe tu”
Maximo huyu ambaye miaka ya nyuma alikuwa anamwaga pesa kwa Marietha na ndugu zake, leo hii anazungumza vitu hivyo,sio siri moyo wa Mama Grace ulichoma kama pasi.Akakata simu na kumueleza Vaileth,kila kitu kilivyokuwa.
Mwezi mwingine baadaye,Maximo akaacha kutuma pesa,mambo taratibu yakaanza kubadilika,Marietha akawa hapatiwi tena matibabu,mirija ya kumpitishia chakula ikawa imekwisha,akawa amefungwa na kamba kitandani,hiyo ilifanya harufu kali itoke ndani ya chumba hiko,ikawa kero kwa majirani.Siku zikazidi kusogea,sawa walikuwa wanaishi kwenye jumba kubwa la kifahari, ambapo hata mtu angeliona angesema ‘Watu hawa hawana shida’kumbe ilikuwa kinyume kabisa.Kifupi maisha yao yakawa kila siku ni afadhali ya jana,mwaka mmoja na nusu baadaye,hali ndiyo ikawa mbaya zaidi kwa wote.
Kilichowashtua zaidi siku hiyo ni baada ya kuona magari yamepaki nje!
“Nyumba ndiyo hii bosi”
Hayo ndiyo mazungumzo yaliyokuwa yanaendelea,watu wanne wakaingia ndani ya jumba hilo na kuanza kuzunguka huku na kule.
“Kwahiyo ushaongea naye?”
Maongezi yakazidi kupamba moto.
“Mimi ndiyo dalali,kuongea na nani sasa?”
“Na mwenye nyumba,maana utapeli ni mwingi siku hizi”
“Mimi ndio Fred Kiluswa,siwezi kukupiga changa la macho kuwa na amani kabisa”
“Basi hakuna tabu,leo nitakulipa nusu.Alafu wiki ijayo,nitamalizia”
“Hakuna tabu”
“Hawa ni nani?”
Mzee huyu tajiri ambaye kwa harakaharaka, alionekana ni mnunuzi wa nyumba,akamuuliza dalali baada ya kumuona Mama Grace na Vailetha wapo nje,wanatumbua macho!
“Usijali,ni ndugu zake bosi wangu”
“Okay,twende serikali za mitaa tukafanye utaratibu”
Hivyo ndivyo ilivyokuwa,ni wazi nyumba ilikuwa inaenda kuuzwa.
Hilo halikuwa na ubishi kwani wiki moja baadaye,walifika maaskari!Mama Grace,Vaileth pamoja na Marietha wakatolewa nje kinguvu na kutupiwa vitu vyao.Maisha kwao yakazidi kuwa mabovu zaidi na zaidi.Huo ndio,ukawa mwazo wa wao kuishi mitaani,wakiwa kama ombaomba,Marietha akiwa hivyohivyo mgonjwa, hana matunzo na alitoa harufu kali sana!

***** ******
Maisha ya Wiliam yalikuwa yaleyale, kupenda vimwana hata alivyoanza masomo yake ya chuo kikuu‘Stockholm University’ nchini Sweden mwenendo wake ulikuwa ni uleule,muda wote yeye aliwaza wanawake tu.Na ilikuwa wazi kabisa,hakuwahi kukataliwa na mwanamke yoyote hata ungekuwa ni nani?Kijana huyu alikuwa ana ushawishi mkubwa na mbinu nyingi sana mbali na hapo uzuri wake pia ulimbeba,alivyofika chuo ndio usiseme,aliwachanganya wanawake kama pilau na kachumbari.Na kitu ambacho kilichowafanya watoto wa kike wamlilie ni moja tu,mwanaume huyu alikuwa anajituma kitandani,ndiyo maana akadiriki kumuopoa mwanamke mwingine anayeitwa Vivian Martin,mtoto aliyechanganyika mataifa mawili,Mexico na Germany.Mwanzo mrembo huyo alionekana kubana lakini baadaye akaachia na siku mbili mbele akawa yupo kitandani na Wiliam mpenda wanawake!
“Do you know how much I love you, Sweatheart”(Unajua ni kiasi gani nakupenda mpenzi)
Wiliam,akiwa yu uchi wa mnyama, juu yake yupo mtoto huyu mrembo Vivian Martin,akamuuliza swali hilo huku akiwa anamtizama machoni kimahaba.
“I don’t know love”(Sijui mpenzi)
“I’ll tell you next time.You beautiful and no word can describe how beautiful you are”(Nitakwambia wakati mwingine,wewe ni mzuri.Na hakuna neno lolote litakaloweza kueleza jinsi ulivyokuwa mzuri)
Wiliam alitoa maneno matamu na baada ya hapo,akamsogelea Vivian mdomoni,akampa ulimi wakaanza kunyonyana midomo kama njiwa,kwa kuwa walikuwa hawana nguo hata moja,ilikuwa rahisi kwa Wiliam kupitisha mkono wake mpaka makao makuu ambapo huko kulikuwa na ikulu,akaanza kushika kinyama kimoja laini hapo ndipo mtoto huyu,akaanza kuvuta vuta mashuka.Ilikuwa ni wazi kabisa,vitu alivyoanza kuhisi havikuweza kuelezeka kwa peni na karatasi,akazidisha kasi ya kunyonya mdomo wa Wiliam,kifua chake kilivyoshikwa akawa hajiwezi tena.Bila kupenda,akachukuwa ndizi ya Wiliam iliyokuwa tayari imesimama dede,akaanza kuichuwa, kwa kuwa ilikuwa tayari imesimama na mgodi wake ulikuwa tayari una majimaji,mwenyewe akajisogeza na kumuingiza nyoka pangoni,kilichofuata hapo,Mimi nawewe hatujui!

***** ******
Ushauri aliopewqa Issa akiwa na Dokta Katrina,uliwaingia akilini kabisa.Waliamini kwamba, kumpeleka mtoto wao akasome barani Ulaya nchini Sweden,ingekuwa sawa sababu huko angekuwa makini mbali na hapo,huko kulikuwa na watoto wengine wa marafiki zao.
“Kwanza atapata Exposure,Karishma ni mtoto mzuri sana.Amekuwa na mpaka alipofikia hapo.Sidhani kama anahitajika kuchungwa tena,anajielewa na sifa zake nazijua”
Huo ulikuwa ni ushauri kutoka kwa Shekh Utali Savimbi,akizungumza na Issa pamoja na mkewe!Issa na Dokta Katrina walimuamini sana kwani mpaka Karishma anafika Chuo,aliweza kutunza Bikira yake, mbali na hapo alikuwa ana fanya vizuri darasani!Hakukuwa na kipingamizi chochote,isipokuwa habari hizo, alivyofikishiwa Karishma,alimwaga machozi.
“Mama siwezi kukaa mbali na nyie.Nimewazoea”
Akagoma,machozi yalikuwa yakimtoka!Hakutaka kukaa mbali na wazazi wake.Mbali na kulia sana,hakuweza kubadili msimamo wa wazazi wake kwamba, ni lazima akasome ‘Stockholm University’Nchini Sweden.Haukuwa utani,mambo yakaanza kupelekwa mkukumkuku!
Baada ya siku tatu matokeo ya Karishma yakawa yametumwa nchini Sweden chuoni,kwa njia ya barua pepe,barua ikajibiwa wiki moja baadaye kwamba amekubaliwa!Mchakato wa kuanza kutafuta 'passport' ukaanza mara moja,ilivyopatikana wakatafuta ubalozi wa Sweden,wakaomba barua ya kujaza Viza.Wakaanza,haikuwa kazi ngumu sababu ilikuwa ni viza ya masomo,siku saba baadaye.Passport ikawa imegongwa viza!Kilichobakia ni Issa na Katrina kulipa ada tu.
“Dad and Mom,hamnipendi”
“Sio hivyo,sisi tunakupenda sana.Ndiyo maana tunafanya hivyo.Tunataka upate elimu ya kimataifa”
“Kwani hapa Tanzania hakuna elimu?”
“Sijasema hivyo mwanangu”
“Kumbe?”
Hapo hawakuwa na jibu.Swala ni kwamba,ilikuwa ni lazima Karishma siku hiyo apande shirika la ndege ya KLM ili aanze safari ya kwenda chuoni,Baba yake alikuwa nyuma ya usukani.Hasemi chochote mpaka walivyofika,uwanja wa ndege wa kimataifa mwalimu Nyerere,usiku huo wa saa nne.Walivyopaki gari,wakashuka na kuanza kutembea mpaka walipokuwa abiria wengine.
“Mwanangu Karishma,usome”
Issa,akaanza kutoa maneno yake,akimwambia Mtoto wake wa kike.
“Dad,nitasoma”
“Mimi vita yangu,ni wanaume.Wanaume ni waongo,wasikudanganye,jitunze sana mpaka uolewe”
“Sawa Dad”
Ilikuwa ni siku ya huzuni kwa Karishma lakini akapiga moyo konde,Mama yake nayeye akatia neno la mwisho.Ilivyofika saa tano,akaanza kutembea kuelekea kwenye lango la abiria wanaosafiri,alivyofika hapo akasimama na kugeuka.Akawapungia wazazi wake mkono,kwa ishara ya kuwaaga huku machozi yakimlenga!



Haikuwa rahisi kwake kukubali kuwa anaachana na wazazi wake na anaenda mbali kabisa,nje ya bara la Afrika.Alitamani kurudi, lakini haikuwezekana,akiwa langoni kuingia ndani ya kimlango kidogo,akazidi kuwapungia wazazi wake mkono kisha kuvua kila kitu,kuanzia bangili,saa na cheni,akatoa na simu yake ya mkononi,akaweka kwenye kikapu maalum,kikawekwa juu ya mashine iliyokuwa inatembea.Akanyanyua na begi akaliweka juu yake,akapita chini ya kimlango ambacho ni maalum kwa ajili ya ukaguzi wa mwisho,hivyo ndivyo abiria wote walikuwa wakipita kwa staili hiyo.Akavuka upande wa pili na kuchukua vitu vyake,akatembea mpaka ofisi za KLM.Ilikuwa ni mara ya kwanza kwake kusafiri kwenda Ulaya lakini alionekana kuwa ni mjanja,kifupi Karishma alijiongeza mwenyewe,alivyofika hapo akamkuta msichana mmoja mrembo,yupo kwenye kompyuta.
“Shikaamooo!”
Karishma, akasalimia.
“Marahaba”
“Naomba kuuliza”
“Uliza tu”
“Tiketi yangu ni hii hapa,sijajua utaratibu upoje”
Dada huyo akiwa katika tabasamu mwanana,akaichukuwa tiketi ya Karishma na kuanza kuangalia.
“Ndege yako inaondoka saa sita,pita pale Immagration ugongewe muhuri,mbele kuna ngazi, upande.Usubiri geti namba kumi na saba”
“Sawa ahsante”
Hivyo ndivyo Karishma alifanya baada ya kupewa maelekezo,kila kitu kilivyokamilika, akapanda ngazi na kusubiri kwenye viti, ambapo huko kulikuwa na wasafiri wenzake,kichwani kwake kulikuwa na vitu vingi sana vikimiminika na mara nyingi sura za wazazi wake zilikuwa zikipita,moyo ulikuwa ukimuuma sana!Lakini licha ya yote, alijipa moyo ya kuwa,ipo siku atakutana nao tena kwani safari sio kifo!Saa sita kasoro na dakika ishirini abiria wanaosafiri na shirika la ndege ya KLM, wakaanza kusimama baada ya kusikia sauti kutoka katika kipaza sauti,hiyo ilimfanya mpaka Karishma nayeye aunge mkia,akatembea na kupita katikati ya bomba kubwa,ambapo huko alikutana na mlango wa ndege,akaonesha tiketi na kuoneshwa siti yake.
“Thank you”(Shukrani)
Karishma akashukuru na kuanza kupita huku akiangalia namba ya siti yake,alivyoipata akapita katikati na kuketi.Ndege, ilikuwa kubwa kupita kiasi na ilikuwa ina uwezo wa kubeba watu zaidi ya mia tano,ndiyo maana abiria walizidi kuingia ndani.Saa sita Kamili mlango wa ndege ukafungwa.Iliyokuwa inasikika wakati huo ni sauti ikitoa maelekezo, ikijirudia rudia kwa lugha tofauti,hapo ndipo ndege ikaanza kusogea taratibu huku abiria wakiambiwa wafunge mikanda yao.Ilivyokaa vizuri ikaanza kutembea taratibu,kadri ilivyozidi kusogea ndipo kasi ilikuwa ikichanganya,ilivyofika kwenye barabara yake kasi ikazidi mno,ikaanza kuunguruma kwa nguvu sana kisha matairi ya mbele yakaanza kuinuka taratibu, ya nyuma yakafuata ikazidi kwenda juu angani huku magurudumu yakijiingiza ndani,kisha ikapotelea angani.Ilivyotulia tu, abiria wakaruhusiwa kufungua mikanda yao,kwani ndege ilikuwa imetulia tayari!
“Hii”
Ni salamu kutoka kwa msichana mdogo wa kichina, aliyekuwa pembeni ya Karishma!
“Hii”
Nayeye akarudisha salamu na kuweka ‘headphone’masikioni,hakutaka stori nyingine zaidi.Ndege, ilitembea angani zaidi ya masaa nane,ndipo walipotua katika uwanja mwingine nchini Amsterdam,hapo walibadili ndege baada ya masaa mengine mawili.Saa sita kasoro na dakika saba,ndipo ndege ilikuwa imefika katika uwanja mkubwa wa kimataifa Arlanda,abiria wote wakafunga mkanda ili ndege hiyo itue nchini Sweden,jijini Stockholm!Ilivyotua,ikatingishika na kukaa sawa,ikazidi kukimbia kwa kasi mpaka ilivyosimama kwenye maegesho yake,maalum.Magari, yaliyokuwa na ngazi yakasogea karibu na mlango,ulivyofunguliwa tu abiria wote wakaanza kushuka!Kila kitu kilivyokamilika,kama kuchukuwa mizigo na kugonga muhuri,Karishma akatoka nje ambapo kulikuwa na watu wengi wanaosubiri wageni wao.
‘KARIBU SWEDEN,KARISHMA ISSA MPELEMBE’
Kibao hiko alikisoma Karishma,kilichoshikwa na mwanamke mmoja mtu mzima, aliyevalia ushungi mweusi,Karishma akasogea na kumshika begani.
“Aasalam aelekuy”
Karishma akatoa salamu na kujitambulisha,hapo hawakuwa na muda mwingine wa kupoteza,wakaongoza mpaka kwenye maegesho ya magari.
“Karibu Sweden Mwanangu”
“Ahsante”
“Mimi naitwa anti Rahma.Umekuwa mdada,mara ya mwisho kukuona ulikuwa mdogo sana,Mama yako ni rafiki yangu!Nilisoma naye India”
“Nashukuru kukufahamu”
Mwanamke aliyejitambulisha kwa jina la Rahma,alikuwa akijaribu kumzoea Karishma ili amtoe wasiwasi,ndiyo maana muda wote alijitahidi kumpigisha stori huku taxi waliyokodi ikianza safari,Karishma bado alikuwa akishangaa mandhari ya jiji hilo, lilivyokuwa zuri,magorofa marefu,treni za umeme zinavyotembea kwa kasi ya upepo!Kwake kila kitu kilikuwa kipya kwani vitu kama hivyo aliviona kwenye luninga tu.
“Tunaelekea Gulumarshplan hotel,ukapumzike kwanza na uongee na Wazazi wako”
“Sawa anti”
Safari hiyo iliwachukuwa dakika arobaini kufika katikati ya jiji la Stockholm,walivyofika walipata hoteli.Wakakaribishwa.
Baada ya Karishma kujimwagia maji akajitupa kitandani,akapewa simu hapohapo ili azungumze na wazazi wake.Alifurahi sana na wazazi wake walimpa moyo na kumtakia masomo mema kwani ipo siku wangeonana tena,hiyo ilimfanya Karishma ajisikie vizuri na kuutua mzigo wa hofu aliokuwa nao moyoni,akajisikia mwepesi na hajatengwa na wazazi wake.Kilichofuata baada ya hapo ni Rahma Juma,kuanza kumtembeza maduka mbalimbali kwa ajili ya kununua makoti na masweta ya baridi sababu kipindi hiko kilikuwa bado ‘summer’ yaani joto,kwa wazungu swala hilo lilikuwa ni sherehe kubwa kwani walikuwa wanadiriki kutembea nje hata na vichupi wakifurahia jua!Kwa Karishma ilikuwa tofauti,hakuzoea bado, alihisi baridi linapenya mpaka ndani ya mifupa yake ndiyo maana akahitaji masweta mengi.
“Mbona hakuna baridi kabisa,Winta ndio kasheshe.Mpaka mabarafu”
Rahma,akampasha habari Karishma wakiwa kwenye duka kubwa la masweta,walivyomaliza wakakata tiketi na kusubiri treni la umeme!Hivyo ndivyo ilivyokuwa na baada ya siku nne,Karishma akaanzishwa chuo,baada ya kila kitu kulipwa!
****** *****
Kitendo cha Karishma kuanza masomo ndani ya chuo cha Stockholm, ilifanya chuo kizima,kitingishike.Ndani ya siku tatu,habari zake zikawa zimevuma kwa kasi ya kimbunga,kila mtu alimzungumzia mgeni huyo ambaye tayari walipata fununu ya kwamba anatokea Afrika,nchini Tanzania.Kila mtu aliyemuona,hakukaa kimya,alienda kumuhadithia mwenzake, jinsi msichana huyo alivyokuwa na uzuri wa ajabu sana,haukuwa utani Karishma, alikuwa ni mzuri kwelikweli na alikuwa amekamilika kila idara, japokuwa alikuwa akivaa nguo ndefu lakini umbo lake lilionekana na kujichora,hiyo ndiyo ikamfanya atie fora na kujichotea umaarufu burebure.
“Ebwanaa eeeh,umemuona mgeni aliyeanza chuo?”
Jamaa mmoja alikuwa akimwambia mwenzake!
“Nasikia sikia tu kuna mgeni”
“Mtoto ana choo hiko”
“Ana choo kivipi?”
“Ana tako kubwa.Kama Nick Minaj”
“Sio kweli”
“Ndio nakwambia sasa,yupo Human Rosource”
“Yupoje?”
“Ebwana eeh,enheeee.Yule pale.Ebu mcheki mtoto alivyoumbika,kama haendi chooni kunya vile”
Haukuwa utani,msichana aliyekuwa wanamteta alikuwa ana uzuri wa pekee,na ilikuwa wazi kabisa ya kwamba haikuwahi kutokea msichana mrembo namna hiyo, ndani ya chuo hiko,ndiyo maana wanafunzi wa chuo hiko kila siku waligongana vikumbo,wakimshangaa hasa hasa alivyokuwa anatingisha yaani Singida Dodoma,Karishma alitokea kunyanyasa vidume wa chuo hiko,kila mtu alitamani ashushe mistari yake lakini ilikuwa vigumu kuzoeleka.
“Mambo”
Ilikuwa ni salamu kutoka kwa mwanafunzi wa kizungu aliyeitwa Mike Damson,akijaribu kumsabahi Karishma siku hiyo, baada ya masomo kuisha!
“Poa”Karishma akajibu kifupi huku akionekana akiwa bize, kupakia madaftari yake ndani ya begi.
“Unaitwa nani?”
“Karishma”
“Una jina zuri,umetokea wapi?”
“Tanzania”
“Tanzania?Ndio wapi?Huko Afrika?”
Mike Damson alitaka kujua nchi ya Tanzania ilipo lakini lengo lake hususani halikuwa hilo,niya yake ilikuwa ni kumvuta karibu Karishma ili amjaze ndani ya kumi na nane zake,amtongoze. Moyo wake ulimsukuma afanye jambo hilo lakini ilibidi afanye ngazi kwa ngazi hatua kwa hatua,asikurupuke.
“Afrika Mashariki”
“Afrika Mashariki pale mimi naijua Kenya na Rwanda,sijawahi sikia jina kama hilo”
“Basi,ndipo nilipotoka”
Kwa Karishma kwake ilikuwa kama kero fulani, ndiyo maana alijibu kwa mkato kwani hakutaka usumbufu wa aina yoyote ile,mbali na hapo alikuwa amechoka na masomo ya siku hiyo.
“Unaishi wapi?”
Bwana Mike,akatupa tena swali lingine lakini Karishma,hakujibu badala yake alivaa begi mgongoni na kuondoka zake.
********
Siku zilivyozidi kwenda mbele ndipo wanaume mbalimbali walizidi kumgasi,hapo nyuma alidhani wenda wazungu hawana tabia hizo za kishenzi na waelewa kumbe walikuwa wasumbufu zaidi ya wabongo!Hilo kwa mara ya kwanza lilimpa tabu,licha ya yote hakuna hata mwanamme mmoja aliyetokea kumtingisha na kumyumbisha,wote aliwachomolea na zawadi alizokuwa anapewa,alizikataa na kurudisha mara moja!
***** ****
Wazazi ama walezi wa Wiliam walijua mtoto wao yupo chuoni anasoma na kulala hostel,jijini Stockholm kumbe haikuwa hivyo.Kijana huyu alikuwa nje ya mji wa Stockholm tena mbali kabisa,alikuwa kijiji kinachoitwa Falun,kwa treni ya umeme inayokimbia kwa kasi ya risasi,ilichukuwa masaa saba ama nane mpaka kufika.Huko hakufata kingine bali wanawake na aliyempeleka jiji hilo, hakuwa mwingine bali ni demu wake mpya aliyeitwa Natasha Billy mtoto wa tajiri anayetingisha jiji la Marekani,huyu ndiye aliyekuwa ndani ya kijiji hiko cha Falun,wanakula bata za kila aina.
“Huu mkufu ni wako mpenzi”
Natasha Billy, alimwambia William huku akimkabidhi mkufu wa dhahabu,Mwanamke huyu hakuwa mwanafunzi bali alikuwa ni msimamizi kwenye biashara za baba yake, aliyekuwa ana viwanda nchini Sweden.Siku moja alivyoenda Chuo kumtembelea mdogo wake ndipo alipojikuta amenasa kwa Wiliam,akampenda sana na alikuwa yupo tayari kumpeleka kwa wazazi wake.
“Nakupenda sana Raphael”
Natasha aliongea kwa hisia zote,wakiwa ndani ya mgahawa wa Mackdonald wanakula baga na sushi,kwa raha zao.
“Namimi nakupenda sana Natasha”
“Nataka unioe”
“Lakini mimi bado nasoma”
“Sitojali”
“Wewe wazazi wako wana uwezo,sisi ni maskini kwetu”
“Hilo usijali”
“Lakini,sidhani kama watakubali mimi ni mswidi wewe ni Mmarekani”
Kila Wiliam alipojaribu kujenga hoja ya kukataa ndoa,Natasha alizivunja kwani alitokea kumpenda sana Wiliam,hakuwa tayari kumuacha na alitamani siku moja aolewe naye,ndiyo maana alitaka ndoa mara moja.
“Mapenzi hayachagui kabila wa uraia mpenzi”
Natasha,akaingizia misemo ili kupigilia jambo lake msumari!Watu hawa walikuwa wenye mahaba mazito,na aliyeonekana kumpenda mwenzake kwa dhati ni Natasha,walivyotoka kwenye mgahawa wakaanza kutembea sehemu tofauti tofauti,pesa kwa mtoto wa kishua kama Natasha halikuwa shida kwake, ndiyo maana wakadiriki kwenda kwenye maduka ya nguo ya gharama,Wiliam akapigwa sop sop!Akafanyiwa shoping ya dola mia nne za kimarekani.Baada ya kutoka hapo wakakodi Hotel,huko ndipo alipotoa shukrani zake wakiwa kitandani,Wiliam alijipinda na kukizungusha kiuno chake ipasavyo, akapeleka spidi nyingi,siku hiyo ndiyo akafanya kufuru.Natasha alitoa miguno na wakati mwingine akawa analalamika kwa lugha ya kifaransa, hiyo ilitokana na utamu wa nanasi aliokuwa nao Wiliam,walivyomaliza hakuamini,bila kusema kitu kingine chochote, akatembea mpaka kwenye mkoba wake na kutoa dolla mia saba,akamkabidhi Wiliam.
“Hii ya kwako mpenzi”
Natasha akasema kimahaba!
“Ahsante mpenzi”
“Bado swala langu lipo palepale.Naomba unioe”
“Tutaongea hilo”
“Raphael,naomba usinisaliti.Nitaumia na siku nikijua una demu mwingine,nitamnyonga kwa mikono yangu”
Natasha, alizungumza maneno hayo huku akitabasamu lakini ni kweli alimaanisha kwani alikuwa ni mwanamke mwenye wivu,alikuwa yupo tayari kutoa uhai wa mtu yoyote Yule ili kulikingia penzi lake kifua!
“Siwezi kukusaliti”
Wiliam akahaidi,siku tatu baadaye wakapanda treni ya umeme ili kurudi jijini Stockholm na Wiliam alivyofika tu,akazama hostel kwake baada ya kuagana na Natasha!

**********
Muda wa kupata kifungua kinywa ulipofika,kila mwanafunzi alikuwa mgahawani.Waliopenda chai waliagiza,waliopenda kahawa walikunywa.Ndani ya mgahawa huo uliokuwa karibu na chuo kikuu cha Stockholm,meza aliyokuwa Wiliam kulikuwa na marafiki zake wawili, ambao walikuwa wanatembea pamoja kila wakati.
“Raphael,kuna mtoto mmoja amekuja hapa chuo.Ni checheee”
Carlos alianza kumwaga sera,akimwambia Wiliam.
“Ah,siku hizi mimi sipandi pandi watoto wa chuo, kwanza wana fangasi!Ninadili na watu wazima tu,wanaojua kulea na kuoga vizuri wakatakata.Huwezi amini, hapa nimejaa balaa,nina kama dola elfu mbili hivi”
“Acha masihara”
“Nakwambia ukweli,kuna duu gani humu anaweza kunipa pesa kama hizi?Zaidi ya stress,watoto wa chuo nimewaachia nyie”
“Lakini umemuona mtoto mwenyewe?”
“Carlos eeh,hapa chuo hakuna wa kunibabaisha!Si,unanijua mimi ni chuma,mwamba”
“Ulikuwa wapi kwanza?”
“Nilikuwa Falun na demu mmoja hivi mtasha,anaitwa Na….”
Wiliam,akasita kidogo.Hakuweza kumalizia sentensi yake,akabaki kinywa wazi, macho yake kayagandisha mbele,ilielekea kuna kitu alikiona kilichomfanya adauwe!Wenzake walivyogeuka,wakatabasamu.
“Demu mwenyewe ndiyo huyo sasa”
“Ndio yule??!”
Wiliam, akauliza kwa mshangao,uzuri wa msichana huyo ulifanya mpaka ahisi damu yake imeacha kutembea kwa kama sekunde tisa!




Ilikuwa ni wazi kwamba William ameuzimikia mzigo,ndiyo maana akawa ameganda kama mtu aliyepigwa na shoti ya umeme, ameduwaa!Anamtizama msichana mrembo ambapo hapo nyuma alikuwa akibisha na kusema kwamba hatotembea na mwanafunzi wa chuo tena.Akili yake ikaanza kubadilika taratibu sababu msichana aliyemuona mbele yake uzuri wake haukuwa na mfano wa kuufananisha na kitu chochote ulimwenguni,ndiyo maana akahisi kama mapigo yake ya moyo yameacha kudunda pia.Karishma alikuwa mbele yake, mita kama nane hivi,amesimama kwenye mgahawa anasubiri kuhudumiwa,kilichomchanganya zaidi Wiliam ni namna ambavyo Karishma, alivyokuwa ana kitu kama kichuguu kwa nyuma,hilo ndilo lilimfanya mpaka damu yake imuende mbio.
Mvulana huyu alikuwa ni kama ana ugonjwa Fulani ama pepo la ngono sababu kila akiona jinsia ya kike ni lazima damu yake imuende kasi na nyoka wake asimame,bila kusubiri chochote mwenyewe akasimama,akatembea mpaka kwa Karishma,kilichokuwa kinamsaidia siku zote ni ujasiri aliokuwa nao, wa kuongea na watoto wa kike,Wiliam hakuwa muoga hasa linapokuja swala la wanawake,hata kama ungekuwa ni wa aina gani, kama amemzimia ni lazima angemfuata bila kuogopa chochote,kifupi hakuwa ana aibu wala haya!
“Mambo kisura”
Wiliam akatupa salamu kwa mikogo huku akitizama huku na kule.
“Poa”
Bila kugeuka,Karishma akajibu na kuchukuwa kikombe cha kahawa,akamvuka Wiliam na kwenda kuketi kiti cha mwisho kabisa pembeni,peke yake.Wiliam,akamfuata na kukaa pembeni pia.
“Naitwa Raphael,Wewe je?”
“Karishma”
“Unasoma hapa?”
“Ndio”
“Umeingia lini?”
“Nina zaidi ya siku nne”
“Umetokea wapi?”
“Afrika,Tanzania”
“Tanzania?Wewe ni mtanzania?”
“Ndio”
“Lakini mbona hufanani nao?”
Karishma,akakaa kimya.Hakujua kwamba, hilo lilikuwa ni swali ama kejeli.
“Oh,samahani.Nilikuwa nina maana ya kwamba wewe ni mzuri sana”
“Ahsante”
“Kwahiyo unaishi wapi?Hapa Stockholm au wapi?”
“Ndio,kule hostel za Bulls”
“Sema ukweli?”
“Ndio huko ninakaa”
“Mimi mbona nipo huko huko”
“Sawa”
Maswali ya Wiliam yalikuwa ni mengi kuliko kawaida na kila Karishma, alipokuwa anajibu maswali,ndipo uzuri wake ulipoongezeka.Alipomuua zaidi Wiliam ni baada ya kutabasamu alivyokuwa anachat kwenye simu,ilielekea alisoma ujumbe uliomfurahisha,hapo ndipo Wiliam akawa hoi bin taaban,akawa hajiwezi tena.
“Naweza nikakuona baada ya masomo?”
William alipendekeza ombi lake.
“Hapana”
“Utakuwa bize bize nini?”
Akajichekesha kidogo kwani jibu alilopewa hakulitegemea.
“Ndio”
“Lini utakuwa frii?”
“Sina frii”
“Basi nitakutafuta”
“Aya”
Karishma hakuwa na ‘time’ na maneno ya Wiliam,kazi yake ilikuwa ni kuweka kikombe cha kahawa mdomoni na kukitoa kisha kuchat,ndiyo maana alikuwa akimjibu William bila ya kumuangalia usoni,alivyomaliza kunywa kahawa,akavuta mkoba wake na kuuweka vizuri.
“Kwahiyo sasa?”
Wiliam alivyoona anaachwa,ikabidi aulize mpango mzima unakuwaje.
“Niko bize”
Karishma, akajibu huku akianza mwendo wake, ambapo huko nyuma ilimfanya Wiliam abaki anakula kwa macho na kushuhudia makalio ya Karishma, yanavyotingishika.
“Duu,hapana.Huyu mtoto ni lazima ajae kingi.Siwezi kumuacha!Mimi ndio Raphael,alafu anaonekana ana kiburi.Hakuna mkate mgumu mbele ya chai hata kidogo.Mimi ndio chai,tena ya maziwa”
Maneno hayo yalipita kichwani kwake,akijaribu kujipa moyo na ushindi wa kumpata kisura huyo, aliyetokea kumpagawisha kwa sekunde chache tu.Rafiki zake,wakafika hapohapo.
“Vipi Raphael?”
Mmoja wapo akamuuliza huku akisubiri jibu.
“Kazi ndogo tu huyu,nilikuwa najaribu kumuweka sawa”
“Yaani Raphael huyu demu ukimpata,nitakuvulia kofia”
“Khaa!Kuna demu ambaye atachomoka hapa kwangu,wewe subiri uone”
“Maana nini unajua,washkaji kibao wamemfukuzia lakini wapi.Sasa,nilikuwa nasubiri urudi jembe langu”
“Mimi ni Jembe,au fagio la chuma”
“Kwani kasemaje,ulimwambia nini?”
Rafiki yake mwingine,alitaka kujua nini alichoongea Raphael.
“Kaka,wewe niachie mimi.Mimi sina maneno mengi,ni vitendo tu.Nipe siku hiziiii,siku hiziii ngapiiii?”
“Mbiliii”
“Ngaaaapi?”
“Mbili”
“Ewaaaaa”
Wiliam aliongea kwa vitendo sababu alisimama na kuonesha vidole viwili na aliongea kwa kusisitiza na kujiamini,hiyo ilifanya marafiki zake wote wamsapoti na kumtia nguvu kuwa, angempata kimwali.Wiliam,alipagawishwa sio mchezo,masomo yalivyoisha tu.Akanyoosha moja kwa moja mpaka hostel,akaulizia ni wapi msichana huyo anaishi,haikuwa kazi ngumu kupajua sababu Karishma alikuwa maarufu hakupoteza muda,akajitosa kimasomaso na kumuibukia mpaka upande wa hostel za msichana huyo,akatembea mpaka mlangoni na kugonga!
“Ngo! Ngoo! Ngooo!”
Wiliam akagonga,akasikilizia ndani kwa kama sekunde saba,ndipo aliposikia mlango ukifunguliwa,sura ya Karishma ikaonekana.
“Ma..mbo ma..mbo, vipi?”
Kigugumizi cha ghafla,kikamvaa.Hakuelewa kimetokea wapi sababu hakuwahi kuwa nacho kabla,hiyo ilitokana na uzuri wa mwanasesere huyu,mbaya zaidi alitoka akiwa amevalia sketi ya mpira inayovutika,ikamchora umbile lake kwa chini.
“Poa”
“Samahani,nimekuvamia bila taarifa.Naweza nikaingia ndani?”
“Hapana,sasa hivi nahitaji kupumzika”
“Kidogo tu,nitie Baraka”
“Kuwa mwelewa kaka.Nimesema nataka kupumzika”
Karishma akaongea kwa ukali kidogo akawa amechomoa,hakuwa tayari kumkubalia Wiliam aingie ndani ya chumba chake,ili iweje yaani?Wakati hakuwa na mazoea naye,hapohapo akafunga mlango huku nyuma akimuacha Wiliam,analamba lamba ‘lips’ zake akizuga na kuangalia huku na kule kama kuna mtu alimwona,alivyohakikisha hakuna watu,akaenda hostel kwake na kujitupa kitandani,hapo hakukaa sawa.Marafiki zake wakaingia,walimuona alipotoka hivyo walitaka kupewa ubuyu!
“Bwana wee!Mtoto anaelewa sasa”
Wiliam,akaanza kuzungumza na marafiki zake huku akisimama na kwenda kwenye friji,ambapo alitoa chupa kubwa ya pombe kali aina ya takira,akachukua glasi tatu na kumimina,akampa kila mtu mvinyo!
“Raphael,imekuwaje kwanza.Maana sio kwa tabasamu hilo”
“Kumbe mtoto ana aibu aibu,mbona ilikuwa rahisi sana.Nilikuwa naye leo geto kwake mule,ngoja niwape mkanda kamili”
Wiliam,hakuwa tayari kuongea ukweli.Alihofia kuchafua Cv yake kwa marafiki zake,hivyo ilikuwa ni lazima atie chumvi na kuweka uwongo.Akapiga fundo moja la pombe na kukohoa kidogo.
“Nilimkuta ametoka kuoga,kanga ndembe ndembe unaambiwa.Nikamwambia ujuwe nini kisura,mimi nimekuzimia…Akaanza oooh sijui mimi nina bwana sijui nampenda kanihaidi ndoa…Nikamwambia tulia wewe hapa mojamoja..Nikamvuta karibu nikampiga denda,akawa anaogopa ogopa”
Wakati Wiliam anazungumza maneno hayo,wenzake wote walikuwa makini kumsikiliza anachosema, wakawa kama wajukuu wanaosikiliza hadithi kwa bibi,haikuwa rahisi kuamini kama Wiliam ameweza kuingia ndani ya chumba chake na kumla denda Karishma, lakini ilibidi wakubali kwani walifahamu fika sifa za Wiliam,hakuwahi kuchomolewa na mtoto wa kike.
“Raphael,hivi una dawa nini?”
“Swaga tu,hakuna uchawi wala nini.Mimi nawapa siku tatu nyingine..Huyu mtoto namuweka nao”
William,alijitapa mbele ya marafiki zake wakati ukweli ulikuwa ni kwamba hata mkono wa Karishma, hakuwahi kuushika.
Hiyo ilifanya kila mtu atamani kuwa Wiliam sababu alikuwa akila vitu vitamu,stori zilivyoisha wakaingia kwenye movie,mara ghafla mlango ukagongwa.
“Nani?”Wiliam,akauliza!
“Isabelle”
Sauti nyororo kutokea nje,ilisikika.Wiliam,akatulia kidogo na kutembea mpaka mlangoni,akafungua.Alikuwa ni msichana mrembo wa kizungu mwenye mwili mdogo yaani ‘English figure’ huyu naye alikuwa katika orodha ya wasichana wake na Wiliam,bila kuuliza chochote wakaanza kunyonyana ndimi.
“Nakupenda Raphael”
Mtoto,akazama ndani.Kilichofuata hapo baada ya salamu kama kawaida ya wanaume wote duniani kote,akiingia demu wa rafiki yao geto, basi kila mtu atatafuta sababu ya kutoka ili mtu,aliwe uroda.
“Raphael,ngoja nipande hostel mara moja.Nimeacha mchuzi jikoni,usije ukaungua bure!”
Hiyo ilikuwa gia ya kuchomoka.
“Sasa kaka,ngoja nimpigie simu Larri Santana.Nakuja nakuja”
Hizo ndizo gia walizotumia kutoka getoni kwa Wiliam,wakimuacha na mpenzi wake wajivinjari.Baada ya mlango kupigwa funguo,Isabelle hakutaka kingine chochote,akamfuata Wiliam mdomoni na kuanza kumyonya huku taratibu mkono wake ukianza kushuka chini makao makuu,ambapo taratibu jogoo wa Wiliam alianza kuwika na baadaye suruali ikatuna kwa mbele,hiyo ilikuwa ni tosha kabisa kwamba pikipiki imewaka, hivyo kinachotakiwa ni Isabelle kupanda na safari ianze mara moja,alichokifanya yeye ni kumsukumiza Wiliam nyuma,akamtupa juu ya kitanda puu!Chali,akapanda juu yake na kuendelea kunyonyana ndimi huku wakivuana nguo moja baada ya nyingine,sekunde tatu baadaye kila mtu akawa kama alivyozaliwa.
“Wil..iam nakupeenda”
Isabelle alizungumza huku macho yake yakiwa yamelegea,hicho ndicho Wiliam alichompendea msichana huyu,macho yake yalivyokuwa makubwa kiasi na malegevu.Msumari, ulikuwa wima umesimama,akajaza mate mdomoni na kuweka tango la Wiliam mdomoni,alivyomaliza hivyo,akapanda juu na kuseti mitambo,Wiliam hakutaka mchezo huo umilikiwe na Isabelle, ndiyo maana akampindua na kumlaza chali,akachukuwa mguu wake mmoja na kuuweka begani.
“Nyoosha huu mguu..Namna hiyo mrembo”
Wiliam,alitoa amri Isabelle akatii,mguu wake mmoja ukawa juu ya bega la Wiliam huku mwingine ukiwa umekunjwa kiasi,Wiliam akaanza kupeleka majeshi majeshi.
“Aaaaah aaaashhh Willia..m fuc** me haaard ooooh yeaaaah,like thaaat..Aaah aaah ashsss”
Miguno hiyo alitoa Isabelle bila kupenda,huku akisikilizia utamu wa nanasi!

**** ******
Shuleni,alimkosa!Na majibu aliyopewa na walimu yalimfanya anyong’onyee!Siku ya pili, alivyofika tena shuleni hapo,swala lilikuwa lilelile kwamba Abraham hajarudi na haikufahamika ni lini atarejea shuleni hapo.
“Kwahiyo hamjui atarudi lini?”
Deo Karekezi alimuuliza mkuu wa shule, baada ya kuambiwa kila kitu kilivyokuwa na jinsi alivyochukuliwa na mzee chonga!
“Kwa kweli hakuwa specific”
“Hana namba nyingine za simu?”
“Ndio hizo ambazo tunazo.Kwani vipi Mr Karekezi,kuna tatizo lolote lile?”
“Hapana,hakuna kitu”
Deo Karekezi,hakutaka kufunguka.Alivyomaliza, kuzungumza akaweka mada nyingine ya namna ambavyo, atapeleka chakula shuleni hapo.
“Wiki ijayo,yatakuja magunia sitini ya unga na matunda yale uliyotaka”
“Hakuna shaka,tutawasiliana”
Hapo hakukuwa na maongezi mengine, zaidi ya Deo kuingia ndani ya gari na kutimua mbio.Alivyofika nyumbani,alimpasha Mtui habari na kumwambia kila kilichotokea.
“Ile ni damu yako Deo,fanya unavyojua ili Abraham,arudi mikononi mwako.Safari hii usikubali kumpoteza”
Mtui,akashauri.
“Nifanye nini sasa?”
“Huyo mzee hapatikani kabisa kwenye simu?”
“Ndio,tangu jana”
“Mmmh,shuleni wanasemaje?”
“Kama nilivyokwambia”
“Hawajakwambia huyo mzee anapoishi?”
“Hawana uhakika na hawajui”
“Cha kufanya,ebu nenda pale shule.Kaulizie alisoma wapi primary”
“Baada ya hapo?”
“Uwende hukohuko shule aliyomaliza standard seven.Nina uhakika utajua pa kuanzia”
“Sawa wacha niende”
“No! Noo! Nooo! Nooo!Subiri kesho Deo”
“Lakini kesho ni mbali Mtui”
“Subira yavuta Kheri”
“Ngoja ngoja yaumiza matumbo lakini”
“Harakaharaka haina Baraka”
Kila mtu akachomeka mithali zake ili kutetea hoja zake.Mtui alikuwa ni rafiki wa ukweli na isingekuwa kuheshimiana Deo angechomoka jioni hiyohiyo.Lakini wakiwa katikati ya maongezi yao,simu ya Deo ikaita, ikiwa ndani ya mfuko wake wa suruali,akaitoa.Akaangalia,namba zilikuwa ngeni,akashusha pumzi kidogo,akaipokea na kuiweka sikioni.
“Samahani,nazungumza na Mr.Deo Karekezi?”
Upande wa pili wa simu ukasikika,ilikuwa ni sauti ya kike.
“Ndio mimi,sijui nani mwenzangu?”
Deo akakubali,hapohapo akaibuka na swali.
“Dokta Katrina.Mke wa Issa Nurdin Mpelembe,tafadhali naomba kuonana nawewe kesho,ni muhimu sana”


Ilikuwa ni shoti ya milioni mia mbili na sabini,baada ya kupiga hesabu za miezi kumi.Jasho lilimtoka Katrina,akawa mwekundu kama ubuyu,yupo nyuma ya meza kubwa pembeni kuna ‘kalkuleta’anajaribu kurudia rudia mahesabu akidhani wenda amekosea,akahakiki tena kwa mara ya kumi na tisa lakini jibu lilikuwa ni lile lile kwamba pesa nyingi zenye thamani ya shilingi milioni mbili na sabini zimepelea,hapohapo akasimama na kutembea mpaka karibu na meza yenye ‘dokumenti’ za mahesabu,akaanza na ‘bid cards’ili ajuwe ni wapi kosa lilipoanzia,alipomaliza ukaguzi wake akazama kwenye ‘draw’ lingine na kuangalia delivery note,hakutosheka akapitia ‘Tax invoices’ zote na malipo yalivyofanyika,hapo ndipo alipogundua kwamba kuna mchezo mchafu ulifanywa,hiyo ni baada ya kulinganisha Tax Invoice na Delivery note.Hakuchelewa,akainua mkonga wa simu.
“Esma,njoo ofisini,ndiyo sasa hivi.Uje na L.P.O zote za mwaka huu”
Ndani ya hoteli waliyojenga yeye na mumewe kulikuwa na ofisi ndogo ambayo ilifanya kila kitu,kuanzia kununua vyakula,vinywaji na kulipia ving’amuzi kila chumba.Na kila kitu kilienda kisomi, kwa sababu kilirekodiwa kwani mali bila daftari huenda bila habari,hivyo ndivyo mwanamke huyu aliyegeukia upande wa ujasiliamali aliamini.
“Keti”
Sura yake ilionekana kabisa kwamba siku hiyo,hakutakuwa na maelewano mazuri.Ndiyo maana msichana huyu Esma,alikuwa akitetemeka sababu alimfahamu vizuri bosi wake,kulikuwa kuna kila dalili ya kibarua chake kuota nyasi siku hiyo, endapo mambo yangeenda vibaya.
“L.P.O ziko wapi?”
“Hizi hapa bosi”
Esma akakabidhi file,kazi ya Dokta Katrina, ilikuwa ni kupitia moja baada ya nyingine.
“Tarehe kumi na saba mwezi wa tano,nani alikuwa zamu?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Katrina,akimtizama Esma Chande, usoni.
“Mpaka nikaangalie bosi”
“Anyway,subiri”
Dokta Katrina,akazama kwenye kompyuta yake na kuingiza tarehe,hoteli yake ilikuwa ya kisasa na ilikuwa ni lazima mfanyakazi akiingia atie sahihi yake na jina lake linaingia moja kwa moja kwenye rekodi zote,hivyo haikuwa ngumu kwake, kumjua ni nani alikuwa zamu.
“Niiitie Araphat na Salim,sasa hivi”
“Sawa bosi”
Esma alivyotoka,akanyoosha mpaka stoo kulipokuwa na vyakula,akawafuata vijana waliokuwa wanapanga maboxi ya soseji na magunia ya unga.
“Mnaitwa”
“Mimi au Salim?”
“Wote”
“Na nani?”
“Bosi”
“Issa au?”
“Dokta”
Kila mtu kinyesi kilimbana,walimuelewa mwanamke huyo, alivyokuwa mkali kama pilipili mbuzi,ni bora angefika tajiri yao mwingine,anayeitwa Issa,ingekuwa afadhali kidogo.
“Kimenuka nini?”
Araphat akamdadisi Esma.
“Bwana mnaitwa,mimi sijui”
Wote watatu wakaongozana mpaka ofisini kwa bosi,ambapo walimkuta anaangalia bado mafaili.
“Shikamoo bosi”
“Nani alipokea oda tarehe kumi na saba mwezi wa tano?”
Katrina akauliza bila kupokea salamu,hiyo iliashiria kuna kila dalili ya kwamba hakuna usalama siku hiyo asubuhi.
“Nimeuliza swali,msiangaliane..Hii sahihi ya nani?”
Hapo alisimama na kuonesha delivery note, ambayo kazi yake ilikuwa ni kuhakikisha mzigo kamili umeingia kwa kutia sahihi, baada ya mzigo kukaguliwa.
“Naomba mnisichezee akili yangu,hii sahihi ya nani?Nitawafunga washenzi nyie!”
“Yangu bosi”
“Nani alileta huu mzigo?”
“Godfrey”
“Una uhakika?”
“Ndio”
“Subiri”
Katrina,hakutaka kulumbana.Hapohapo akainua mkonga wa simu, moja kwa moja akapiga SK meat supplies,baada ya sekunde mbili akawa kwenye laini na mkurugenzi wa kampuni hiyo ya kusambaza nyama.
“Mr.Cheka..Ndio ndio za kazi? Sasa….nina shida kidogo,naomba niangalizie tarehe kumi na saba mwezi wa tano L.P.O namba 000234 mzigo wa shilingi milioni mbili na sitini,nani alileta hapa..Ni God?Sasa naomba umuulize vizuri,alafu nitakupigia simu”
Mkonga wa simu ulivyowekwa chini,akawatizama.
“Sikilizeni niwaambie,msinifanye mimi ni mtoto mdogo”
Siku hiyo Katrina,akaibua sekeseke ofisini.Na dakika mbili baadaye akapigiwa simu na kuambiwa ukweli kwamba,Bwana Godfrey hakuleta mzigo walikula njama na pesa ziliingia mifukoni mwao.
Dokta Katrina,akapandwa na jazba,akapiga simu polisi na wafanyakazi wote wakachukuliwa na kuwekwa ndani kwanza mpaka uchunguzi mwingine ufanyike,Shoti nyingine ilitokana na sheli ya mafuta,hiyo ilimfanya azidi kuogopa zaidi na zaidi.Alivyoenda kwenye hospitali yake binafsi,mambo yakawa yaleyale.
Alivyochoka zaidi ni baada ya kusikia duka lake la dawa,limeingiza shoti pia.
“Eh Mungu wangu,nini hiki?”
Alitafakari siku hiyo mpaka basi.Hakuelewa ni mkosi gani unatokea kwani alikuwa ni mwanamke anayesali swala tano,siku hiyo ya Ijumaa akataka kujua ni kitu gani hakipo sawa,ndipo akanyoosha mpaka kwa Shekh Maarufu nchini Tanzania aliyeitwa Shekh Seleman Yakuti,akapaki gari Magomeni mapipa!Alivyoonana naye,akamuadithia kila kitu,hapohapo ubani ukachomwa Shekh akaanza kupiga dua.Alivyofumbua macho tu,akamuangalia Katrina Usoni.
“Kuna mtu mmemkosea sana,inabidi mumuombe msamahaa na mumrudishise mali zake.Subbanah Allah, hawezi kupokea dua zako.Kuna mtu kati yenu bado ana visasi wewe ama Mumeo,dua zako haziwezi kufika hata kidogo.Quaran inasema samehe ndipo Dua yako itafika”
Katrina alisikiliza kwa umakini mkubwa sana,picha iliyomjia kwa harakaharaka kichwani kwake ni Deo Karekezi,ilikuwa ni lazima mali zake walimrudishie, pamoja na fedha ambazo alitapeliwa na Issa kwa kuuza mali zake.Ni kweli, baada ya kutoka Kwa Shekh Seleman Yakuta,akaingia nyumbani kwake akimsubiri Issa kwa wudi na uvumba,amwambie ukweli na ikiwezekana walimrudishie mali zote za Deo Karekezi,pia wapatane.
“Vipi?”
Issa aliingia siku hiyo na kukumbana na mkewe yupo seblen,amekaa juu ya kochi.Uso wake ukionesha kabisa kwamba kuna kitu fulani ambacho,hakikuwa sawa.
“Issa,mali za watu tutarudisha lini?”
“Za nani?”
“Deo Karekezi,kesi alishinda.Inabidi alipwe pesa,pesa zake pia.Lini lakini?”
“Atapewa tu”
Issa alijibu, kana kwamba jambo hilo lilikuwa la kawaida,akapuuzia na kuingia ndani.Hiyo ilimfanya Katrina achukie zaidi,akaingia chumbani nayeye,ambapo hakumkuta Issa,ni wazi kwamba alikuwa bafuni anaoga,alivyoangalia juu ya kitanda,akaona simu.Akaisogelea na kufungua,cha kwanza kufungua ni meseji ambazo alizisoma lakini moja ilimshtua ni baada ya kuona mpango Fulani wa kumuuwa Deo,jambo hilo lilimuogopesha sana.
‘BADO TUNAMFUATILIA’
‘SIPENDI HILO JIBU,MIAKA MINGI IMEPITA.MNANIAMBIA HIVYO HIVYO,VP?HAMUWEZI KAZI?’
‘HAPANA BOSI,HUYU MTU HAKUWEPO DAR,LAKINI AMEFIKA TAYARI’
‘YUKO WAPI?’
‘YUPO DAR,ANAISHI TEGETA PALE KWA MZEE MMOJA ANAITWA MTUI,KARIBU NA KWA SWAI’
‘SASA MNASUBIRI NINI?’
‘KAULI YAKO’
‘NATAKA HUYO DEO KAREKEZI AFE,KESHO KESHO VAMIENI PALE.KWANI HIYO NI KAZI YA KUTUMIA DAKIKA NGAPI?’
‘DAKIKA SIFURI BOSI,KESHO TU NITAKUPA TAARIFA NZURI’
‘FANYA HIVYO’
Katrina, alikuwa akisoma meseji hizo huku akitetemeka mwili,aliogopa kuliko kawaida, hakutegemea kama Issa amegeuka kuwa jambazi muuaji,mambo hayo yeye alizoea kuyaona kwenye filamu tu.Akili yake ikafanya kazi kwa kasi ya upepo, aka ‘scrinshot’ meseji zote,akajitumia kwenye simu yake, mtandao wa ‘WatsApp’haraka akarudi seblen huku akitafakari ni kitu gani akifanye,ilikuwa ni wazi kwamba asubuhi ya siku inayofuata,ilikuwa ni lazima Deo afe endapo atofanya kitu chochote kile,alishaanza kumuogopa pia Issa,akaumiza akili yake ni kitu gani akifanye lakini akashindwa.
“Nipige simu polisi,hapana”
“Nifanye nini sijui?”
Dokta Katrina,akazidi kutafakari zaidi na zaidi,akijiuliza ni kitu gani akifanye.

***********
Majambazi waliotumwa na Issa kumuuwa Deo Karekezi, walikuwa tayari wamefanya uchunguzi wao na kugundua kwamba mtu huyo anaishi Tegeta,mbaya zaidi walijua mpaka mtu anayeishi naye anaitwa Mtui.Kazi yao, ikaonekana kuwa rahisi kuliko walivyodhani kwani walikuwa wakimsaka Deo kwa miaka mingi sana bila mafanikio,walivyojua anapoishi, hawakutaka kufanya tena makosa,na nafasi hiyo kwao wakaiita ‘GOLDEN CHANCE’yaani nafasi ya dhahabu kwa lugha ya kiswahili.Mikakati kabambe, ikapangwa na ilikuwa ni lazima siku hiyo asubuhi sana wavamie nyumba ya Mtui,Deo apigwe risasi afe mara moja kisha watokomee zao.
Kazi hiyo ilionekana rahisi zaidi baada ya kutumiwa kiasi cha shilingi milioni tatu kama nusu ya malipo ya kazi yao,salio lililobaki lilikuwa ni milioni tatu nyingine, hiyo ilikuwa ni baada ya kumaliza kazi yao.
“Kesho asubuhi,kabla jogoo hajawika”
Huyu alikuwa anaitwa Kimboka,alionekana kuwa ndiye mkuu wao wa kazi kwenye kundi lao.
“Pale kwani kuna mlinzi?”
“Kuna masai tu, ana kirungu”
“Basi shega,huyo atapigwa nakozi moja tu”
“Safari hii tusifanye makosa”
“Haitotokea”
Mpango wa kumuuwa Deo,ukawa tayari umekamilika na kikao kilifungwa baada ya kuhaidiana kwamba Deo auwawe saa tisa za usiku.
Saa nane nusu,wakaamshana na kuingia ndani ya gari wakiwa na silaha zao mikononi kwenda kumuuwa Deo,kwao pesa ilikuwa mbele kuliko utu.Milioni sita kwao ilitosha kabisa kutoa uhai wa binadamu mwenzao,nusu saa baadaye walikuwa tayari wameizunguka nyumba ya Mtui na kuiweka katikati,wakavaa vitambaa usoni na kutoa bastola zao.
“Kacha kacha!”
Mlio wa bastola kukokiwa,ukasikika.

**********
Mpaka inafika saa sita za usiku kitu usingizi kwa Dokta Katrina, kilikuwa ni hadimu kupatikana,kichwa chake kilijaa msongo wa mawazo,hiyo ikasababisha mpaka presha ipande.Alivyoona hivyo akaenda jikoni na kukata kitunguu swaumu,akameza na maji ili presha yake ishuke.Kichwani, alimuwaza Deo Karekezi,aliamini kwamba mwanaume huyo akifa Allah hatomsamehe na mali zake kivyovyote vile zitafilisika kwani damu ya mtu haiendi bure,masaa siku hiyo yalikuwa yakienda kwa kasi mithili ya maporomoko ya owen falls,kushtuka ilikuwa ni saa nane kasoro mbili, bado alikuwa anausumbua ubongo wake,tayari alishamuogopa Issa.Na aliogopa zaidi kwani Issa alikuwa tayari anamiliki bastola,hiyo ikamfanya awe na hofu mno.
“Hapana,kwanini uogope?Wakati mali ni zako,lazima upaze sauti.Katrina paza sauti,sema ukweli wewe ni mwanamke jasiri,usiogope”
Sauti hiyo ya ndani kwa ndani,ilimsumbua.Hapohapo ikampa nguvu na ujasiri wa hali ya juu,akanywa fundo la maji na kuanza kupanda ngazi mpaka chumbani,akaufungua mlango kwa jazba zote,akamkuta Issa anachati yupo kitandani.
“Una nini?”
Issa akauliza huku akitoa simu pembeni,ilionekana alishtuka.
“Nipe simu yako Issa”
Katrina akaongea huku akitetemeka.
“Ya nini?”
“Kuna mtu nataka nimpigie mara moja”
“Kwani simu yako iko wapi?”
“Haina vocha”
“Tigo au Voda?”
“Voda”
“Nakutumia salio”
“Nina shida na simu yako”
“Shika”
“Hapana sio hiyo,nipe iphone”
“Katrina,mbona sikuelewi?”
“Naomba simu yako Issa”
Issa akawa kama ana hanya,akaonekana kuwa ana wasiwasi kuliko kawaida,akachukua simu aina ya Iphone na kumpa Katrina,mwanamke huyu hakuchelewa akazama inbox kutafuta meseji lakini cha kushangaza hakukuta meseji,hiyo ilimfanya ashtuke zaidi lakini kwa upande mwingine alijipongeza kwani bila ku ‘scrinshot’ ingekula kwake.
“Lini umeanza hii tabia?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Katrina,akihema kwa jazba!
“Tabia gani Honey?”
“Nisikilize nikwambie Issa,hapa nilipo nina RB yako.Chochote kitakachomkuta Deo.Nitakufunga yaani hata aking’atwa na nyoka.Kwanini hutaki kumsamehee kwani bado unampenda mke wake? al..”
“Katrina mbona sikuelewi?”
“Hunielewi nini jambazi mkubwa wewe,nataka talaka yangu leoleo…Siwezi kuishi na jambazi...Nimekwambia ukweli,unajua nini nina maanisha.Wapigie simu wakina Kimboka waambie,wasitishe wanachokifanya la sivyo Issa.Hii Dunia utaiona chungu,mpigie Kimboka sasa hivi…”
Katrina aliongea kwa jazba na hasira zote, mapafu yake yakajaa hewa,kifua chake kikawa kinapanda juu na kushuka,amevimba kama chura,damu yake inamuenda mbio kutokana na hasira zilizompanda kwa kiasi cha kutosha,hiyo ilimfanya mpaka Issa aogope, mbaya zaidi alipewa simu ambayo ilikuwa na meseji zote walizochat na watu wake huo ulikuwa kama ushahidi tosha uliosomeka wamuuwe Deo Karekezi.
Hapo ndipo jasho lilianza kumtoka Issa,akaona milango ya gereza inafunguka na kutupwa ndani kwa kosa la kutaka kufanya mauaji.
“Ukai…maliza kuwapigia nataka tala…ka yangu,TUACHANE SIWEZI KUISHI NAWEWE TENA”
Dokta Katrina alimaanisha.Na alitaka jambo hilo lifanyike dakika hiyohiyo.
“Au nipige simu polisi,nipige simu polisi nakuuliza?”
Issa,alikuwa anafokewa kama mtoto mdogo siku hiyo,akahisi mwili wake umepungua uzito ghafla.Hapohapo,akawapigia simu vijana wake wasitishe mpango wa kumuuwa Deo kwani ilikuwa tayari kitumbua kimeingia mchanga,vijana wakasitisha zoezi lao,Dokta Katrina akawa ameyaokoa maisha ya Deo Karekezi.
“Naomba niandikie talaka yangu,mimi na wewe basi”
Katrina akasema na alimaanisha,sababu usiku huo hakulala chumbani na Issa.Akaingia chumba alichokuwa analala Mtoto wake Karishma,ambaye alikuwa yupo nchini Sweden kimasomo,huko alilia mpaka kunakucha,akatoka bila kumuongelesha Issa na kuanza safari ya kuelekea ofisini kwake akiwa ana mawazo tani elfu saba,kichwa chake kilikuwa kizito kama kobe.
Alivyofika akatulia mpaka ilivyofika jioni,akamtafuta Deo Karekezi hewani.
“Ni muhimu Mr.Deo.Njoo hapa Kariakoo,Big bon…Kama unakuja Kariakoo Sokoni..Sawa kama unapafahamu”
Katrina alikata simu,akashusha pumzi ndefu,hakuamini kama amezungumza na Deo,alishukuru Mungu sababu alimuokoa kutoka kwenye kifo.Akavuta kabati la chini na kutoa karatasi!Alivyoipitia,akaona kwamba Deo anadai shilingili milioni mia tatu na hamsini,hapohapo akasimama na kutoka mpaka nje kwa sekretari.
“Kuna mgeni wangu atakuja hapa,anaitwa Deo Karekezi.Utamwambia apite tu”
“Sawa bosi”
Akaitikia,msichana mrembo wa kihindi.

*** *****
“Ndio Katrina,kanipigia simu”
“Katrina yupi?”
“Si,Yule dada wa kihindi.Yule wa mahakamani al…”
“Basi nishamkumbuka.Anataka nini?”
“Niende kumuona”
“Utaenda peke yako?”
“Ndio”
“Una uhakika?”
“Kwanini unauliza hivyo Mtui?”
“Si unajua maelewano yenu sio mazuri,tafuta mtu uwende nae lolote linaweza kutokea”
“Usijali Mtui,wacha nikamsikilize.Huyu dada sidhani kama ana niya mbaya”
“Aya”
Deo,akatoka nje akawasha gari na safari ya kwenda Kariakoo kuanza mara moja,alivyofika baada ya dakika arobaini baadaye,akawa tayari ameingia ofisi za Big bon!Alivyotaja jina lake,akaambiwa apite moja kwa moja,akasukuma mlango wa kioo na kukumbana na harufu ya unyunyu wa kihindi,ofisi kubwa nyuma ya meza amejaa mwanamke huyo wa kihindi,ilikuwa ni tofauti na miaka ya nyuma alivyomuacha akiwa bado binti mdogo,Katrina alinawiri na kuwa mnene mnene!
“Karibu Mr.Deo”
Katrina,akasema huku akitoa tabasamu pana na kusimama kwa heshima,wakapeana mikono!Kisha Deo akaketi kwenye kiti kimoja wapo cha wageni.
“Za masiku?”
“Nzuri”
“Pole kwa matatizo”
“Nishapoa”
“Uko wapi siku hizi?”
Katrina akauliza,lakini Deo alionekana kama hataki maswali sababu hakumjibu,aliishia kumwangalia na kutulia tu.
“Anyway..Tuna deni lako nimekuita hapa tujue tunalipana vipi,leo nitakupa milioni mia moja na hamsini.Kisha the rest, tutajua itakuwaje”
Deo,akapigwa na mshtuko mkali pili alishindwa kuelewa kama amesikia vibaya ama ni kweli,hakuwa anakumbuka kama alikuwa anadai deni kubwa namna hiyo,kutokana na ‘stress’alizokuwa nazo kichwani,hiyo ilimfanya ashtuke na kumtumbulia macho Katrina utadhani, mjusi aliyebanwa na mlango!



Maisha kwao yalikuwa yakutanga tanga kila kukicha,shida ziliwaandama kila siku.Kwao ilikuwa kila siku ni afadhali ya jana,maisha yao yakawa yamegeuka ghafla kutoka kwenye maisha ya starehe mpaka dhiki tena ghafla mno,mbaya zaidi,mzigo mkubwa kwao alikuwa ni Marietha, ambaye alikuwa kama mfu aliye hai,alikuwa akitoa harufu mbaya ya kutisha,matumizi ya kifedha waliyokuwa wanapewa na Maximo kusafisha taka mwili za Marietha,zilikata hazikutumwa tena!Ndiyo, maana alitoa harufu kali kupita kiasi,mbali na hapo ndugu zake Mama Grace na Vaileth, waliendelea kumtunza Marietha,walijitahidi kumpa chochote walichokuwa nacho, lakini kadri siku zilivyozidi kwenda mbele walioneshwa kushindwa na kuchoka kabisa.
“Nataka kwenda Arusha”
Siku hiyo Mama Grace,alimwambia Vaileth baada ya kufika katika kibanda kidogo, walichokuwa wanaishi.
“Kwenda Arusha?Kufanya nini?”
Vaileth, akauliza.
“Kutafuta maisha”
“Maisha gani? Mama Grace”
“Wewe mtu, akikwambia kutafuta maisha,unamwelewa vipi?”
“Sina maana hiyo”
“Una maana gani?”
“Nina maana kwamba,tuna mgonjwa”
“Huyo mgonjwa wewe si upo?”
“Mama Grace”
“Ndio Jina langu,alafu usinichanganye kabisaaaa,mimi naondoka zangu.Ninaenda Arusha kutafuta maisha nishakwambia”
“Sasa unaniacha mimi mwenyewe”
“Kila mtu afe kivyake,ndiyo maisha ya mjini”
Mama Grace alikuwa akiongea maneno hayo, akiyamaanisha kwani alikuwa akiweka nguo zake vizuri ili aondoke kwenda jijini Arusha kuanza maisha mengine mapya,hakutaka kubaki tena Lushoto.Alisahau, yeye ndiye alikuwa chanzo cha Marietha kuanza mahusiano na tycoon Maximo.
“Huo mzoga baki nao mwenyewe”
Mama Grace alimaliza na kuondoka zake huku nyuma akimuacha Vaileth na Marietha,huo ndio ukawa mwanzo wa matatizo mengine kuanza!Marietha,alikuwa katika taabu kubwa na aliendelea kuwataja watoto wake kila siku akidhani wamekufa,alikuwa ana kila dalili ya kwamba akili yake imeharibika tayari,ndiyo maana wakati mwingine alikuwa akizungumza mwenyewe.
“Mimi…Abraham na Wiliam…Tutaenda kwa baba…Hapana Abraham wangu Wiliam”
Marietha siku hiyo, alikuwa akiongea huku akiwa ameshika mdoli,anauongelesha, nywele zake chafu sana zipo timtim,mwili wake umejaa ukurutu.Ungepewa picha yake akiwa miaka ya nyuma na kuambiwa huyo ndiye yeye Haki ya Mungu vile ungebisha,mwili wa Marietha ulikongoroka,akawa mwembamba,nyama zote zilipotea akabaki mifupa mitupu.
Mwezi mmoja baadaye hali ikazidi kuwa mbaya zaidi kwani alianza kutoka nje na kutembea barabarani,kikaibuka tena kibarua kingine cha Vaileth kumrudisha ndani.Lakini siku tatu baadaye,Marietha hakuonekana nyumbani.Vaileth,akachanganyikiwa!Hakukata tamaa,akazidi kumtafuta kila pembe lakini hakumuona Marietha,alichoamua baada ya siku nne kupita,akaenda kuripoti polisi, faili la kupotelewa na ndugu yake likafunguliwa,baada ya hapo akarudi nyumbani.

Marietha,tayari maisha yake yalihamia jalalani,akawa anashinda anashika makopo na kuwakimbiza watu huku akiita majina ya watoto wake,hilo lilikuwa ni jibu tosha kwa watu wanaopita barabani, kumnyooshea vidole na kumpa jina ‘chizi’hayo ndiyo yakawa maisha ya Marietha kuanzia siku hiyo,kazi yake ilikuwa ni kuzunguka zunguka huku na kule, akizungumza mwenyewe!
****** *****
Deo Karekezi,hakutaka kuamini kama pesa alizoambiwa zitaingizwa kwenye akaunti yake ya benki.Siku hiyo alimuona Katrina kama malaika vile,kwake pesa hizo zilikuwa ni nyingi sana!Mbali na hapo, alikuwa tayari amezisahau,ndiyo maana mapigo yake ya moyo yalipiga kwa nguvu sana,bado hakuamini jambo lililokuwa limetokea, lilikuwa ni halisi,alidhani yupo ndotoni na muda mfupi atashtuka, japokuwa hakutaka iwe hivyo.
“Yes,usha transfer?Baada ya siku ngapi?Naomba nitumie hiyo slip kwenye email yangu.Okay ahsante”
Dokta Katrina, alikuwa ameweka mkonga wa simu sikioni,anazungumza na upande wa pili.Alivyoweka mkonga chini,akamtizama Deo.
“Done!”(Tayari)
“Ahsante sana”
“Pole na usumbufu”
“Usijali dokta”
“Hukuniambia unajishughulisha na nini siku hizi?”
“Biashara ya mahindi na matunda”
“Unauza mahindi?”
“Nauza mahindi na Unga”
“Una supply au?”
“Yes”
“Mbona hukuaniambia mapema?Nina hoteli siku hizi.Naweza nikakupa tenda?”
“Tenda?!”
Deo akauliza kwa mshangao,hakutaka kuamini.
“Ndio tenda”
“Sawa”
“Basi,naomba uje kesho asubuhi sana.Nitaongea na watu wa procurement office, acha akaunti namba zako.Kampuni yako imesajiliwa Gipsa?”
“Ndio nilisajili”
“Nitakupa oda,hope bei zako ni nafuu”
“Kabisa”
Deo akawa amepata tenda nyingine ya kupiga mkwanja,alivyorudi nyumbani akampasha Mtui mambo yalivyokuwa,Mtui akaonekana kufurahi kupita kiasi,hakuamini kama mambo yangekuwa namna hiyo.
“Mungu ni mkubwa sana”
“Ni kweli”
“Mimi nina amini safari moja,huanzisha nyingine.Kwa sababu bila kuanza biashara ya mahindi nadhani nisingeonana na Abraham”
“Kabisa”
Siku hiyo walipiga stori na ili kunogesha zaidi wakatoka nje ya nyumba.Nyumba ya Mtui ilikuwa na uwanja mkubwa kwa nje, ambao ulipambwa vizuri na katikati kulikuwa na mti wenye taa,hapo waliweka viti na meza juu wakaweka chupa ya Wisky,taratibu wakaanza kujipongeza na kukumbushiana mambo mengi ya ujana, yaliyopita na changamoto za kimaisha,hapo ndipo wazo la Deo la kununua kiwanja na kujenga, likamjia.
“Ndio,ni wazo zuri Deo.Tena ukilipwa lifanyie kazi.Haraka iwezekanavyo!”
“Hilo halina shida..Cheeeeeers”
Wote wakasimama na kugongesha glasi zao, zilizokuwa na vileo ndani yake.
“Cheeeeeeers”
Wakasema kwa pamoja tena na kuziweka mdomoni.
***********
Ilikuwa ni lazima Abraham asafirishwe kwenda mkoa mwingine ili Mzee Chonga amuweke mbali na mzee anayeitwa Deo Karekezi,akiamini kwamba anataka kumtenganisha na Abraham, mtoto ambaye alimlea kwa nguvu zake zote,haikuwa rahisi kukubaliana na swala hilo ndiyo maana alimchukuwa shule ili akakae naye kwanza nyumbani.
Niya yake ikiwa ni kutafuta shule nyingine,kwa muda wa siku nne nzima alikuwa akitafuta ufumbuzi wa tatizo lake.Hakuelewa huku nyuma ilikuwa furaha kwa Mama Maria, ambaye alikuwa akijichofyea kibuyu cha asali kwa raha zake,Abraham alikuwa akienda kwa Mama Maria kila siku,kumshughulikia ipasavyo,akimpa dozi.Kutokana na utundu wa Abraham na kujituma kwake kitandani,mama huyo akambatiza jina la kumuita ‘Bedroom professional’ yaani mjuzi kitandani,hakuna siku aliyochanganyikiwa kama siku hiyo.
Miguu yake miwili, ilikuwa imepanuliwa huku na kule.Abraham anamimina asali katikati ya mgodi,akapaka paka kidogo.Kisha akaweka kikopo pembeni,akainamisha kichwa chake na kuanza kulamba mgodi ambao juu yake ulikuwa na asali,hiyo ilimfanya Mama Maria,aishiwe nguvu na wakati mwingine, alihisi mapigo yake ya moyo yameacha kutembea.Ulimi wa Abraham ulikuwa katikati ya mgodi wake,akawa anajikunja kunja na kuvuta mashuka,utamu ulivyozidi akawa anakishika kichwa cha Abraham na kukikandamizia kwa ndani ili asimwache,hiyo ilimaanisha alikuwa anakaribia kufika, safari yake!
“Aaaaah aaah Abr..haaam yeeess aaaah hiv..vyooo ashiiiii aashiiiii”
Hiyo ndiyo ikawa miguno ya Mama Maria,akiwa ameyafumba macho yake anasikilizia utamu wa mtoto huyu.Kwa Abraham,picha lilikuwa bado halijaanza kwani kama ni mechi ndiyo kwanza alikuwa anavaa jezi ili aingie uwanjani,sio siri mtoto huyu alikuwa kungwa kwenye mchezo huo ambao hauhitaji nguvu wala hasira,alivyomaliza kulamba mgodi,akasogeza ulimi wake kwa juu kidogo na kukigusa kitu kilichofanana na kiharage,hapo ndipo Mama huyu alipohisi roho yake inaacha mwili,alipomuua kabisa ni baada ya mkono mmoja wa Abraham kupita juu ya chuchu zake.
“Aaaaah aaashiii”
Mama Maria,akaanza kuzungusha kiuno chake kwa kasi,Abraham akajua nini maana yake.Hakutaka, Mama Maria ashinde goli huku yeye akiwa bado anapasha,juu kwa juu akapiga mpira kwa kichwa akazama uwanjani hapohapo ili kusawazisha goli la Mama Maria, ambalo tayari alikuwa amelifunga.Abraham nayeye akaingiza wachezaji wake,filimbi ikapigwa.Uwanja ulikuwa tayari umelowa hivyo ilikuwa rahisi kwa wachezaji wa Abraham kuteleza na mpira kiulaini,Wakaanza kunyonyana denda huku mkono mmoja wa Abraham ukiwa kwenye nido za Mama Maria,hapo ndipo Mama huyu akaanza kuhisi kupasha upya,hakukaa hata sekunde saba,mtanange ukaanza upya.Mechi ikaanza kuchezwa,pasi zikaanza kupigwa.Mama Maria,akapata tena nafasi ya kuchonga kona,bila kuchelewa mpira ukaendelea kuchezwa bao la pili likapatikana.
“Shika hapaaa”
Abraham,akasema huku akiwa ana hema kwa mbali,jasho la usoni linamtiririka kimtindo.
“Wa...api Baby?”
Mama Maria,akauliza.Macho yake yalikuwa yamelegea sio mchezo,ndiyo maana hakusikia vizuri.
“Shika hapa,weka huu mguu hivi”
“Hivii?”
“Hapana,uweke hivi”
Mzee mzima Abraham,akawa ameshika miguu ya Mama Maria yote miwili,akaingia kati na kuweka mpira ndani,pasi zikaendelea kugongwa.Kiuno cha Abraham kilikuwa kinazunguka kila pembe ya mgodi,akawa anakinyonga kana kwamba hana mifupa,kazi yake ilikuwa ni kupitisha mpira kila pembe ya uwanja.
“Ah ah ah ah ahaaa beib...iii ashii ashiii aah aah”
Miguno ilizidi huku kitanda kikisikika kikinesa,mtoto huyu alikuwa akitoa dozi sio mchezo.Dakika sita baadaye,ndipo Abraham akafanikiwa kupachika goli la kwanza,akatulia juu ya kiuno kwanza ili kusikilizia.
“Tuendelee?”
Abraham,akauliza.
“Haapaaana,tupumzike kidogo.Nina kiuu ya maji”
Ilikuwa ni lazima,aombe mapumziko la sivyo siku hiyo angeweza kuzirai kitandani.
“Abraham”
Mama Maria akaita kwa jicho la huba.
“Naam mpenzi”
“Leo umeninywea Viagra?”
“Ah wapi?Kwanini?”
Abraham,akauliza kwa makusudi.Alijua dozi aliyompa, lakini alitaka tu asifiwe kidogo.
“Leo hii,umenikomesha.Tangu nianze kukujua,sikuwahi kupata vitu kama hivi.Kweli wewe ni BEDROOM PROFFESIONAL”
“Si unakumbuka leo nimekula vizuri,nikanywa maji mengi na maziwa”
“Kumbeeeeeeee?”
“Ndio,vitu hivi vinahitaji uwe umeshiba vizuri maji mengi kwa sana”
“Mimi nilikuwa sijui”
“Nakutobolea siri”
Mama huyu hata siku moja hakuwahi kudhani kama kuna siku angeenda mizunguko zaidi ya kumi kwa muda mfupi,alibaki akimwangalia Abraham bila kummaliza,alikuwa ni mdogo kwake lakini hakujali.Wakati mwingine alitamani mumewe angekuwa na nguvu alizokuwa nazo, mtoto huyu mdogo wa umri.
“Uliniambia Baba yako,anataka kukuamisha shule?”
“Ndio love”
“Anakupeleka wapi?”
“Sijajua”
“Nataka kukupa zawadi”
“Zawadi gani?”
“Simu,lakini make sure baba yako hajui.Tutakuwa tunawasiliana.Siku ukitaka kuondoka niambie”

***** ******
Ilibidi atumie jiwe moja,kuuwa ndege wawili kwa wakati mmoja.Yaani amsake Mwanaye Abraham huku akiwa anatafuta kiwanja cha kununua kwani baada ya siku tano kupita akaunti yake ikawa imecheua mamilioni ya pesa baada ya kulipwa na Dokta Katrina,Deo Karekezi meno yake yalikuwa nje wakati wote!
“Inabidi ninunuwe usafiri wa kutembelea,si eti Mtui?”
Deo Karekezi akaomba ushauri,ingawa swala hilo alikuwa nalo kichwani.
“Hilo ni muhimu kwa sasa hivi”
“Gari gani,itanifaa unadhani?Mimi nishazeeka sasa”
“Inabidi utafute gari ya hadhi kidogo,wewe ni mfanyabiashara.Inabidi kidogo,uwe na mkwara watu wakuheshimu”
“Eti eeh?”
“Ndiyo maana yake”
“Kuna jamaa yangu mmoja,ametoka japan juzi.Ana yard ya Magari.Nitampigia simu baadaye”
“Sawa sawa.Pia inabidi niongeze Fuso nyingine”
“Maliza moja kwanza,ndio uanze na lingine ndugu,mbona una pupa hivyo?”
“Sina mtu wa kunipa mawazo sasa”
“Tafuta mwanamke wa kuishi naye,awe anakusaidia kwa sasa hivi”
“Hilo nalo neno,kuna mwanamke nimemuona mtaa wa pili hapo.Ni mzuri sana!”
“Achana na wanawake wa mtaani hawa,watakusumbua.Watakufirisi,wanawake wa sasa hivi,wajanja sana.Usipokuwa makini ndugu yangu,utarudi nyuma kimaendeleo”
“Sasa unataka kuniambia nini?”
“Jambo hilo fikiria mara mbilimbili kabla hujaamua”
“Sawa,nitatafakari”
Maisha ya Deo,yakawa taratibu yanarudi kwenye mstari.Kila siku alikuwa ni mtu wa kujishughulisha,aliwaza pesa na kutaka kufungua vitega uchumi vingine kama kufungua mafremu na kuyakodi,huo ndio ulikuwa mpango wake wa kwanza endapo angepata kiwanja,kwa kufanya hivyo aliamini angejenga nyumba yake.Na hapo angeenda kuchukuwa mkopo benki,kisha ajenge hosteli za wanafunzi wa chuo.Usiku wa siku hiyo alikuwa akipitia daftari ambalo huandika mipango yake.
“Hili nitalifanya baada ya kupata kiwanja.Maisha ni mipango bwana”
Akajitupa kitandani na kulala.

**********
“Kuna kiwanja huku”
“Wapi?”
“Korogwe”
“Korogwe?”
“Ndio mzee wangu”
“Naweza nikakiona leo?”
“Ndio unaweza”
“Sawa basi,nitakuwa huko jioni jioni”
“Sawa mzee wangu”
Deo,alimaliza Mazungumzo,akiwa ndani ya gari lake,kali tena ya kisasa aina ya Volks Wagen, ambayo alitokea kuipenda, ndiyo maana akainunua.Kwanza ilikuwa imevimba kila sehemu na ‘luxury’ vilevile.Gari hiyo, ilimtoa ushamba mpaka Mtui kwani gia ya gari hilo haikuonekana kwa macho.
“Deo,hili gari umeshalizoea?”
Mtui,aliuliza kila wakati kila alipoliona gari hilo, linaingia ndani ya geti lake.
“Bwana wee,ushamba mzigo.Nishaizoea tayari,gia yake ipo hapa pembeni ya usukani,una press tu.Kama hivi”
Siku hiyo Deo akageuka kuwa mwalimu.
“Kweli nimepitwa na wakati”
“Mambo ya kisasa haya,kila siku mambo yanabadilika.Tunatakiwa tujifunze kila siku”
“Kabisa,hizi ndiyo funguo zake?”
“Ni kama rimoti.Hii gari inawashwa kwa kidole”
“Bwana wee,aisee”
Siku hiyo asubuhi nzima walipoteza muda wao,kulizungumzia gari la Deo ambalo lilikuwa na siku sita tangu linunuliwe.
“Alafu nitaenda Korogwe leo,Yule dalali kanipigia simu.Kapata kiwanja”
“Vizuri sana,inabidi uwende.Korogwe si hapo tu”
“Twende wote Mtui,ndugu yangu”
“Sasa De..”
“Nakuomba”
Hakukuwa na kipingamizi,mikakati ya safari ikaanza mara moja.Hakukuwa na haja ya kupaki nguo kwani ilikuwa ni lazima warudi siku hiyohiyo.Walivyooga,wakaingia ndani ya gari,Deo akaweka kidole kwenye sehemu maalum, gari ikawaka.
Safari ikaanza hapohapo,ndani ya masaa matano, wakawa wameingia mkoani Tanga,wilaya ya Korogwe.
“Uko wapi sasa?”
Deo akazungumza simuni,akitaka kujua dalali wa kiwanja, alipo.
“Msufini”
“Ndio wapi?Mimi sipajui bwana”
“Kwani upo wapi mzee?”
“Stendi ya mabasi”
“Uliza,boda boda wa hapo Msufini,ukifika Msufini nipigie simu”
“Okay”
Deo alivyokata simu,akateremka kutoka ndani ya gari,akauliza vijana waliokuwa juu ya pikipiki zao,akaelekezwa.Alivyorudi ndani ya gari,akaanza safari.Akaingia,ndani ndani,akakunja kushoto na kuacha barabara ya lami.Kuanzia hapo Deo Karekezi,akapunguza mwendo wa gari huku akiwa ana kwepa mashimo,gari yake ilikuwa mpya,ndiyo maana akawa anakwepa makorongo,alivyofika eneo lililoitwa msufini,akaweka gari kando na kupiga simu.
“Sasa,ebu ulizia kwa Mangi mchinja mbuzi”
“Mangi naniiiiii?”
“Mchinja Mbuzi”
Bahati nzuri,kuna mtu alikuwa anapita pembeni,hapohapo akateremsha kioo.
“Kijana, samahani kidogo”
Deo,akasema.Kijana aliyekuwa anapita,akasimama ili kusikiliza.
“Habari yako?”
“Nzuri,shikamoo”
“Marahaba,nauliza kwa Mangi mchinja Mbuzi.Ndio wapi?”
“Mangi Mchinja Mbuzi,Mangi mchinja Mbuzi..Unaona hii barabara...Sasa Nyooka nayo,kona ya kwanza,ya pili ya tatu kushoto.Ndio hapohapo”
“Ahsante sana”
Safari,ikaanza tena.
“Deo”
Mtui,akamuita Deo huku akionekana kama ni mtu anayetaka kumwambia kitu fulani.
“Yes?”
“Yule Mama unamkumbuka?”
“Yupi?”
“Yule pale,ameshika kiuno”
Moyo wa Deo,ukapiga kwa nguvu.Kwanza,hakuamini na pili hakuwa ana uhakika kama mwanamke anayemuona pembeni, ameshika kiuno ni Vaileth.
“Vaileth!”
Deo,akasema kwa mshangao,akaweka gari kando,akashuka na kumsogelea mwanamke huyo, aliyeonekana amepigwa na maisha.Akamsogelea karibu kabisa,Deo hakuwa Yule wa kipindi kile ametoka jela,amemfuata Vaileth akiwa mwenye nywele chafu ananuka shida,siku hiyo alikuwa amechomekea,mkanda nje kitambi kimechomoza,chini amevaa moka ya bei mbaya,akamsogelea vaileth na kumshika bega.
“Vaileth”
Vaileth,akaonekana kama mtu aliyepigwa na bumbuazi,akawa anamwangalia Deo kama mtu anayefananisha kitu ambacho hana uhakika nacho!
“Wewe ni…”
“Deo,Deo Karekezi”
Hapo ndipo moyo wa Vaileth,ukapiga mkambo.Akalitizama gari lililokuwa pembeni ya Deo la gharama sana,kwake jambo hilo lilikuwa kama muujiza mkubwa mno!
“Deoooo,Mungu wangu”
Vaileth,akaita kwa mshangao wa waziwazi.Alitamani kumuomba walau shilingi mia moja,lakini alijishtukia,tumbo lake lilikuwa na njaa.
“Ndio Mimi,unafanya nini huku?”
“Ninamtafuta Marietha”
“Unamtafuta Mariethaaa?”
“Ndio,Marietha”
“Kakwambia anaishii huku siku hizi?”
Hapo ndipo Vaileth,akalazimika kusema kila kitu kilichotokea na maisha ya Marietha yalivyokuwa kwa ujumla.
“Deo,nisaidie kumtafuta Marietha.Niliambiwa huwa anaonekana huku.Karibu na shule ya msingi Kilimani”
“Ndio wapi?”
“Kule juu”
Deo,akatafakari kidogo.
“Sawa,pole sana.Twende!”
Katika maisha yake,hakupanga kabisa na hakufikiria kuonana na Mwanamke anayeitwa Marietha lakini siku hiyo,alishindwa kujuwa ni kwanini amefanya jambo hilo.Walivyoingia ndani ya gari,ilibidi Deo amwambie Mtui mkasa mzima kwa kifupi,ndipo safari ya kwenda shule ya Kilimani ikaanzia hapo.
Ni kweli,wakawa kama wametabiri kwani mbele yao walimuona mwanamke mchafu mwenye masizi usoni,ameshika makopo mkononi.
“Yule pale”Vaileth akasema huku akinyoosha kidole.
Deo,akashtuka.Moyo,ukamuuma kupita kiasi!Hakuamini kama mwanamke anayemtizama ndiye huyu aliyefunga naye pingu za maisha kanisani,akashuka ndani ya gari ili kumuangalia vizuri!
“Mariethaaa…”
Akaita kwa sauti ya chini huku akimshangaa, kuanzia juu mpaka chini.Vitu vingi vikawa vinapita ndani ya kichwa chake,Mtui nayeye akashindwa kubaki ndani ya gari,akafungua mlango ili ashuhudie vizuri.Ni kweli,mwanamke aliyekuwa mbele yao,alikuwa ni Marietha,sio Mtui wala Deo,hakuna hata mmoja wapo kati yao aliyekuwa yupo tayari kukubali kwamba mwanamke huyo ni Marietha!
“Wiliam,nitakuchapa…Nyamaza unyonye…yoyoyo yoyoyo.Abraham,unalia nini..Kimanzi chana kuleeee….”
Marietha alikuwa akizungumza mwenyewe huku akiwa ana kopo mkononi,akilifananisha kopo hilo na mtoto.Deo,akazidi kusogea karibu zaidi huku akimshangaa Marietha,akajikuta roho inamuuma sana.



Bado haikumuingia akilini mtu yoyote yule,sio Deo wala Mtui.Kila mtu alipigwa na butwaa la waziwazi,haikuwezekana hata kidogo kwa Marietha kukumbwa na hali kama hiyo.
“Mpakie kwenye gari”
Deo alizungumza maneno hayo kwa uchungu,hiyo ilimfanya kila mtu amshangae yeye.Alichosema,ndicho kilichofanyika kwani Marietha alishikiliwa na kuingizwa ndani ya gari kilazima.Kichwani mwa Mtui na Vaileth, kulizunguka vitu vingi sana, kila mtu alikuwa anajaribu kumtafakari Deo ni binadamu mwenye roho ya aina gani,ni wazi kwamba, Marietha hakustahili kusamehewa, wala kukaa karibu Deo,hiyo ni kutokana na unyama aliomfanyia huko nyuma.Mtui, alitaka kuzungumza kitu lakini akasita kidogo!
“Kuna hospitali yoyote ya karibu hapa?”
Deo akauliza huku mlango wa upande wa dereva ukiwa wazi,kichwa chake kipo ndani anamuuliza Vaileth aliyekuwa viti vya nyuma na Marietha.
“Hapo nyuma kuna hospitali ndio”
“Nataka,akaogeshwe kwanza.Avae nguo safi alafu mengine yatafuata.Mtui,mpigie simu Yule dalali mwambie tutaonana naye ndani ya dakika ishirini ama thelathini”
Deo alizungumza hivyo kwa kumaanisha sababu aliingia ndani ya gari na kulipiga nolinda,alivyohisi limekaa sawa akazungusha usukani na kurudi alipotoka!Niya yake ikiwa ni kutafuta hospitali ya karibu,kichwa chake kilisongwa na mawazo kila alipopiga jicho kwenye kioo cha katikati na kumuona Marietha, yupo nyuma anazungumza mambo yasiyoeleweka,moyo ulimuuma ajabu,hakuelewa ni kwanini anatoa msaada huo, sababu aliapia ya kwamba hatokuja tena kuishi na shetani kama Marietha,lakini siku hiyo mambo yalikuwa kinyume chake,alihisi kumsaidia kwani aliamini yupo katika mateso makubwa sana.
Dakika kumi baadaye wakawa wamefika hospitali ya wilaya ya Korogwe,wakamteremsha Marietha mpaka mapokezi.Hapohapo, wakaitiwa muuguzi!
“Nahitaji msaada wako kidogo”
Deo akasema huku akimtoa muuguzi pembeni.
“Msaada gani Baba angu?”
“Nina mgonjwa,ninahitaji umuogeshe.Kisha umtunze hapa,nitakuja baada ya muda mfupi,najua hii ni nje ya ofisi lakini nitakupa kitu kidogo”
Deo alizungumza akimuangalia muuguzi huyu usoni,alivyomaliza akachomoa pochi na kutoa shilingi elfu sabini,hiyo ilikuwa ya kumsafisha Marietha na kumpaka dawa za kutoa bakteria wote, waliokuwa mwilini mwake.Jambo hilo lilivyokamilika,akarudi ndani ya gari akiwa na Mtui.
“Deo,kuna kitu leo nimejifunza kutoka kwako.Alafu sikukijua katika maisha yangu”
Mtui alianzisha maongezi baada ya gari kuanza kugeuzwa.
“Kitu gani?”
“Kwa kitendo hiki ulichokifanya.I’m proud”
Kuanzia hapo Deo hakujibu kitu chochote,safari ya kwenda kuonana na dalali ikaanza hapohapo,haikuchukuwa muda mrefu, wakawa wamefika na kuoneshwa kiwanja kilipo.
“Heka ngapi hizi?”
“Heka elfu moja”
“Heka Elfu moja?Kiwanja hiki kimepimwa?”
“Ndio,nyaraka zote ninazo. Alafu kuna mzee mmoja kigogo, anakitaka hiki kiwanja,nimekataa pesa yake kwa ajili yako.Cha kufanya kinunue haraka”
Kama kawaida, maneno ya madalali yanakuwa mengi katika biashara zao,vitu aliyokuwa anaongea vilikuwa tu ni kachumbari ili amtingishe mteja wake,amuuzie kiwanja.
“Usimuuzie,by this week nitakupigia simu”
“Hakuna shaka”
“Serikali za mitaa ni wapi?”
“Hapo nyuma”
“Inabidi,nifanye taratibu zote nikija.Nionane na mwenyekiti wa serikali za mitaa”
“Karibu sana”
“Ahsante”
Mazungumzo yakawa yamekomea hapo kwa siku hiyo, wakiwa na mihadi ya kwamba wataonana tena hata kabla ya wiki moja nyingine kupita,walivyoingia kwenye gari safari ikawa ni kurejea tena hospitalini kumuona Marietha,walivyofika wakaambiwa wasubiri kwanza kwani alikuwa anasafishwa na kunyolewa nywele zake kisha baadaye apakwe dawa na kuchomwa sindano ya anti-biotic.
“Hapa karibu kuna duka la nguo?”
Deo akamuuliza Vaileth.
“Ndio,lakini kule stendi”
“Shika,nenda kununue nguo.Hii utapanda pikipiki”
Hivyo ndivyo ilivyokuwa,Vaileth akapewa pesa na kutoka nje,safari ya kwenda kununua mavazi ili avalishwe Marietha ikaanza kwani isingewezekana kwa yeye kuvaa tena nguo zilezile chafu, wakati alikuwa ametoka kusafishwa.Dakika mbili baadaye Vaileth,akawa amefika tayari na mfuko uliojaa nguo mbili tatu.
“Hizi hapa”
“Waambie,wamvalishe hizo”
Kilichosemwa na Deo ndicho kilichoenda kufanyika,Marietha akawa msafi,nywele zake zimekatwa vizuri,amevalishwa nguo mpya,akaingizwa kwenye wodi la wagonjwa,akafungwa vizuri na mikanda.Deo,akaitwa ili akamuangalie.Kitendo cha kufika,alitamani kudondosha chozi,Marietha alikuwa amechoka,mwili wake umekongoroka kwa kiasi cha kutosha,hakuwa Yule Marietha wa nyuma,mwenye mwili mnene,nyuma ana mzigo mkubwa wa kuvunja chaga.Deo,akasogea karibu na kumshika kichwani.
“Naomba nisamehee Mke wangu,najua yote nimesababisha mimi”
Deo,akasema kwa uchungu,alikuwa ana kila sababu ya kuongea maneno hayo.Ulikuwa ni ukweli mtupu,yeye ndiye chanzo,kwani ndiye aliyemfukuza Marietha nyumbani kwake.Na ndiyo maana alikuwa ana kila sababu ya kumuomba msamahaa mke wake wa ndoa,mbali na kumchukia kwa kipindi cha nyuma lakini alijikuta anarudisha moyo nyuma,ilikuwa ni kama filamu ya kuigiza siku hiyo.
“Marietha….”
Deo akaita lakini Marietha,hakuwa mwenye habari yoyote ile.Alikuwa akizungumza maneno yasiyo eleweka.Deo,akainama kidogo na kumpiga busu Marietha kwenye paji la uso wake,hiyo ilimaanisha bado kuna chembechembe za mapenzi ndani ya damu yake,haikuwa uwongo alihisi bado anampenda mkewe wa ndoa aliyekula naye kiapo kanisani atakuwa naye kwenye shida na rahaa, mbali na hapo alitaka jukumu la kuzirudisha akili za Marietha alivae yeye,hakutaka kukumbuka ya nyuma tena,alichotaka yeye ni Marietha apone,warudi kama zamani.Daktari alivyoitwa,ilibidi aanze vipimo,mara moja.Baada ya nusu saa majibu yalitoka kwamba Marietha akili yake imeathirika kisaikolojia,hivyo anahitajika mtu aliyebobea na kucheza na akili yake.
“Hapa,anahitajika Dokta wa saikolojia.Hii kazi ipo nje ya taaluma yangu”
“Kwahiyo anaweza akapona?”
“Kupona atapona”
“Itachukuwa muda gani?”
“Kwa kweli sijui,angekuwa ana malaria hapo ningekuwa nina uhakika.Lakini hilo swala na mimi ni vitu viwili tofauti”
“Ahsante dokta”
“Karibu tena”
Baada ya mazungumzo hayo kumalizika,Deo akatoa pochi mfukoni na kulipa deni la hospitali.Ilibidi alipie pia ‘bedrest’ sababu alitaka Marietha atunzwe kwanza hospitalini hapo ili yeye arudi mjini Dar es salaam kutafuta waatalam,ambao wangeweza kucheza na akili za Marietha!
Shukrani alizotoa Vaileth,zilishindwa kuelezeka,alishukuru mpaka machozi yakamlenga,bado alishindwa kumfananisha Deo na kiumbe chochote kile duniani,alikuwa ni mwanamme wa kipekee na alikiri kusema ya kwamba alishawahi kuishi na binadamu wa aina nyingi lakini Deo hakuwa binadamu wa kawaida.
“Ahsante sana Deo,Mungu akubariki.Akuongezee.Ahsante sanaaa baba”
Vaileth alishukuru zaidi ya mara sitini,akiwa nje karibu na maegesho ya magari.Deo, alikuwa anataka kuanza safari ya kurudi jijini Dar es salaam.
“Safari njema Deo,ahsante sana.Mungu atakubariki tu na ufike salama”
“Amen,Amen.Hakikisha tunawasiliana,kitu chochote kikitokea.Nipigie simu,namba zangu anazo dokta Msuya”
Deo,alihitimisha maongezi na kufungua mlango wake wa gari akaingia,akalitia moto na kuanza kuondoka,alivyoangalia ‘site mirror’ ya kulia akamuona Vaileth akiwa amesimama, anapunga mkono huku akiwa kama mtu aliyepigwa na bumbuazi.
*******

Jukumu la kuzirudisha akili za Marietha ili awe kama binadamu mwenye akili timamu, akalivaa kama lilivyo,hakujali ni kiasi gani cha pesa litamgharimu,ndiyo maana muda wote alikuwa akipiga simu na kuuliza ni wapi angepata daktari wa saikolojia,usiku na mchana alihangaika.Na hakuacha kupiga simu Korogwe kujua hali ya Marietha,Mtui hakutaka kumuacha rafiki yake kipenzi nyuma,akawa naye bega kwa bega kuzunguka huku na kule ili kutafuta madaktari.
“Deo,Dokta Katrina ulimtafuta?”
Baada ya siku tano kuzunguka na kupiga simu mbalimbali,siku hiyo Mtui akaibuka na jina la Dokta Katrina.
“Ayaaa!Umenikumbusha kitu.Ngoja nimtafute sasa hivi”
Alichokisema ndicho alichokifanya,hapohapo akaruka hewani na kumtafuta Dokta Katrina, kwenye laini, alivyompata akanyoosha swali lake moja kwa moja.
“Dokta wa Saikolojia?”
Dokta Katrina,akatupa swali simuni.
“Ndio”
“Ninaowajua mimi wapo watatu lakini kuna mmoja,ambaye ni the best”
“Utanisaidia vipi?”
“Ngoja nizungumze naye,nitakupigia simu”
“Nikupe muda gani?”
“Dakika kumi”
“Sawa”
Deo,akawa tayari amepata mwanga! Matumaini yake yote, yakaegamia kwa Dokta Katrina,dakika tisa baadaye simu ikaita na aliyekuwa akipiga ni Dokta Katrina,habari zilikuwa ni njema ya kwamba.Dokta amepatikana!
“Anaitwa dokta Filbert Makalla.Ni mzuri sana kwenye saikolojia”
“Unasema ukweli?”
“Trust me”(Niamini)
Dokta Katrina na Deo Karekezi,wakageuka na kuwa marafiki wakubwa sana.Mipango ya kukutana na Dokta Filbert Makalla, bingwa wa kucheza na akili za binadamu wenzake,likafanyika ndani ya siku mbili katika hotel ya New Afrika Hotel.Deo hakuficha,akasema shida yake.
“Huyo mgonjwa yuko wapi?”
Dokta Makalla,akauliza baada ya kusikiliza kila kitu,alitaka kumuona mgonjwa atakayeenda kumtibu.
“Yupo Korogwe”
“Nitaweza kumuona vipi?”
“Itabidi aje Dar es salaam”
“Akishafika,nitafute kwenye simu”
“Okay”
Dokta Makala kwa makamo, alikuwa mwenye umri kati ya miaka 35-48,hakuonekana kuwa mzee wala kijana lakini alijiamini kuweza kufanya kazi hiyo, kwani alizungumza kwa ujasiri kupita kiasi.Jambo la kwanza likawa tayari limekamilika,kilichotakiwa kufuata ni Marietha, kusafirishwa mpaka jijini Dar es salaam.
“Atafikia kwangu Deo,usijali”
Deo alivyomwambia Mtui kwamba Marietha atafikia hotelini ndilo jibu alilompa.
“Hapana Mtui,sasa nitakuwa nawasumbua”
“Deo mimi ni nani yako?”
“Rafiki yangu”
“Hapana! Mimi ni ndugu yako,sisi ni kama ndugu sasa.Hata siku moja sitoweza kusahau ulivyonitoa kwenye umaskini mpaka nipo hapa.Kama ukitaka urafiki wetu ufe,Mpeleke Marietha hotelini”
“Lakini Mtui,unajua kabisa tatizo la Marietha,sasa atakaaje humu ndani?”
“Deo,nadhani hujanielewa.Nasema kwamba,Marietha atafikia hapa kwangu full stop.Nini maana ya undugu sasa?”
Siku hiyo jioni,uliibuka mzozo mkubwa sana,ikawa vuta n’kuvute!Deo, hakutaka Marietha afikie kwa Mtui sababu aliogopa kumtwisha mzigo mwingine,kwa Mtui nayeye hakutaka Marietha akafikie hotelini.
Muafaka waliofikia ni kwamba Marietha afikie nyumbani kwa Mtui,ndiyo maana dada wa kazi akaanza kusafisha chumba ambacho kilikuwa kitupu,kikapigwa usafi na kudekiwa vizuri kwani kesho yake Marietha alitakiwa kufikia ndani ya chumba hiko.
Katika swala hilo Deo alijitoa mzima mzima bila kujishauri,kulivyokucha siku iliyofuata, akawasha gari kwenda Korogwe,Mungu akawa yupo upande wake kwani alifika ndani ya masaa matano!Alivyofika tu,hakutaka kupoteza wakati kwani alitakiwa kugeuza siku hiyohiyo.
“Muweke vizuri,mfunge mkanda huo.Sio hivyo..Subiri”
Deo akatoa maelekezo,Marietha alivyokuwa anaingizwa ndani ya gari lake,alivyoona wanakosea ilibidi ateremke ili amfunge mkanda wa gari Marietha.
“Mbona ametulia leo?”
Deo akamuuliza dokta!
“Tumemchoma sindano,nilitaka nisahau.Kuna dawa nitakupa,kama mkipata daktari.Amchome ili hali yake itulie”
“Sawa hakuna shaka”
Deo akapewa maelekezo mengine na kupewa dawa!Kila kitu kilivyokamilika,akapiga gari moto,safari ya kurudi jijini Dar es salaam ikaanza mara moja.
Deo alihisi mgongo unamuuma, kutokana na kuendesha gari kwa muda mrefu sana,mbali na kuchoka hakutaka kulala njiani, ilikuwa ni lazima siku hiyo afike Dar es salaam hata kama angechelewa,ndani ya gari walikuwa wapo watu watatu tu.
Deo,Marietha pamoja Vaileth.Saa, kumi na moja ya jioni, ndipo waliwasili nje ya geti la Mtui.
“Piii piiiiiii”
Mlio wa honi,ukasikika.Geti likafunguliwa!Deo, akaingiza gari ndani,mpaka sehemu maalum,akatokeza Mtui na mkewe.
“Poleni na safari”
Mtui,akawa karibisha.Hapo ndipo walipomtoa Marietha na breki ya kwanza wakampeleka chumbani.
“Huyu ni Marietha?!!”
Mke wa Mtui,akauliza.Afya ya Marietha ilimfanya aulize kwa mshangao!
********
Mikono ya Mke wa Mtui ilikuwa shingoni mwa Marietha usiku wa manane,anamkandamiza kwa nguvu zake zote akiwa juu kitandani,niya yake ikiwa ni kumnyonga afe kabisa kwani alitokea kumchukia sana!
Kutokana na Marietha kufungwa kamba mikononi na miguuni,hakuweza kushindana nguvu na Mke wa Mtui,akabaki anatingisha tingisha miguu,ni wazi kwamba alikuwa anakata rohoo!Mke wa Mtui, aliendelea kukandamiza shingo ya Marietha,ambayo ilifanya hewa ishindwe kutoka na kuingia ndani ya mapafu,akazidi kukukuruka.
“Kufaa Malaya wewe”
Mke wa Mtui, alikuwa akisema maneno hayo huku mishipa ya kichwa ikiwa imemsimama kwa hasira,alikuwa yupo tayari kuuwa.Dakika nne, zilikuwa nyingi kwa Marietha kwani alitulia tuli,akaacha kutingisha miguu.




Mtui, alikurupuka kutoka kitandani kama mtu aliyemwagiwa maji ya baridi,ndoto aliyoota ilimtisha kupita kiasi.Kwamba mkewe alikuwa akimnyonga Mke wa Deo kitandani,asilimia themanini na tano ya ndoto yake ilikuwa inaendana na ukweli kwani historia ya Marietha na mkewe huko nyuma zilikuwa ni mbaya,kifupi Mke wa Mtui na Marietha hawakupipika chungu kimoja.Japokuwa, siku zote Mke wa Mtui alimuonesha tabasamu Marietha, lakini siri hiyo nzito alikuwa nayo Mtui kwani alishawahi kumtamkia wazi wazi kwamba anamchukia Marietha, mbali na hapo alitaka kumfukuza nyumbani hapo kipindi cha Deo, alivyokuwa anakula Msoto gerezani,alivyojaribu kuunganisha mambo mbalimbali, ikamfanya apate hofu nyingi.Alivyopeleka mkono wake juu ya meza na kuwasha taa ndogo,akaogopa zaidi kwani mkewe hakuwepo kitandani.Kama mjeshi,akachomoka na bukta yake fupi na kufungua mlango wa bafuni, akidhani wenda mkewe yupo humo anajisaidia lakini hakukuwa na dalili ya mkewe kuwepo,kijasho chembamba kikaanza kumtoka,akanyonga kitasa.Alivyotokeza kwenye korido,akaona taa ya jikoni inawaka,akatembea taratibu na kumuona mkewe yupo na nguo ya kulalia tu,amefungua friji ameshika glasi ya maji ya kunywa.
“Vipi?”
Mtui,akahoji huku akimuangalia mkewe kwa macho Fulani ya wasiwasi sana.
“Nimekuja kumeza dawa,presha ilikuwa juu sana”
“Mbona hukuniamsha?”
“Sikutaka kukusumbua mme wangu”
“Ushakunywa sasa hizo dawa zenyewe?”
“Ndio”
“Twende basi tukalale”
Hapo wakaongozana na Mtui,akazima taa ya jikoni.Wakaingia chumbani,ndoto aliyoota Mtui ilikuwa bado inampitia kichwani na alijaribu kuitafakari inamaanisha nini.Wakati mwingine, alidhani wenda Mkewe ameshamnyonga Marietha usiku,akajishauri aende chumbani kwa Marietha ama asiende.
“Marietha amelala?”
Mtui akamuuliza mkewe.
“Sasa mimi nitajuaje?Mimi ndio inabidi nikuulize wewe”
“Sikuuliza kwa niya mbaya lakini”
“Namimi sijakujibu kwa niya mbaya”
Mtui,hakutaka kuuliza tena swali lingine zaidi.Aliogopa kumchefua mkewe, ambaye huwa hapendi kulisikia jina la Marietha,kuanzia hapo usingizi ukawa kitu hadimu sana kupatikana kwa Mtui,mpaka kunakucha.
Alichofanya baada ya kupambazuka, ni kugonga chumba cha Marietha huko aliamini kivyovyote vile, Deo angekuwepo!
“Za asuhuhi Deo?”
“Nzuri tu karibu”
Sauti ya Deo iliitikia kutoka ndani ya chumba,mlango ukafunguliwa.
“Vipi mgonjwa?Anaendeleaje?”
“Mambo si haba,ndio nataka kwenda kuonana na Yule mtaalam leo”
“Mungu ni mwema,Marietha atapona.Amini nachokwambia”
“Natamani iwe hivyo”
Baada ya kila mtu kuoga na kupata kifungua kinywa,Deo akachukuwa simu na kumtafuta Dokta Filbert Makalla, hewani.
“Ndio TMJ hapa”
“Nije na mgonjwa?”
“Ndio,njoo naye.Tuanze kazi mara moja”
Alichosema Dokta Makalla ndicho kilichoenda kufanyika,Vaileth na Deo pamoja na Marietha wakaingia ndani ya gari huku nyuma wakiachana na Mtui kwani yeye alikuwa anaenda kutafuta mkate wake wa kila siku,wakaachana barabarani.
Gari la Mtui likaelekea Magharibi,Deo akakunja Kaskazini kwa ajili ya kwenda hospitali ya TMJ!Marietha alikuwa kimya kabisa,haongei chochote, isingekuwa sindano aliyochomwa wenda angekuwa anapiga kelele,jicho la Deo mara nyingi, lilikuwa nyuma,kila alipomuangalia Marietha,alihisi uchungu ajabu!Moyo wake ulihisi kumsaidia na alitaka kusahau yote, yaliyopita nyuma kwani mambo yote aliyatafsiri kama changamoto katika maisha kwani aliyachukulia maisha ni kama safari ambayo siku zote inakuwa ni ndefu na imejaa mabonde na milima,mbali na hapo aliamini pia Marietha ndiye mke aliyepewa na Mungu.
“Ngoja tupitie huku Sinza,tutokee Shoppers plaza”
Deo alizungumza mwenyewe,baada ya kufika Mwenge mpakani,akazungusha usukani na kuchukua barabara ya kuingilia Sinza.Ambapo,dakika nane baadaye, aliibukia barabara ya Makumbusho,akanyoosha na kukunja kona ya mtaa wa Dokta Kairuki,akanyoosha moja kwa moja na kuibukia Mikocheni.Alivyokamata barabara kubwa,haikumlia muda sana,akawa tayari ameshafika TMJ.Akaweka gari kando na kumtafuta Dokta Filbert Makalla simuni,akamueleza ujio wake.Hazikupita hata dakika mbili,Dokta akatokeza na kuwataka waingie ndani na mgonjwa!
“Ulisema hali hii ilianza lini?”
Dokta,akaanza maswali,wakiwa ndani ya ofisi ya Dokta Makalla.Deo,alishindwa kujibu, Vaileth akalivaa swali hilo na kuanza kusema kila kitu kilichotokea nyuma,mpaka walivyomkuta Marietha nje ya geti.
“Yaani,yeye ni kutaja hayo majina tu?”
Dokta,akaibuka na swali jingine.
“Ndio”
“Hao watoto wake,wako wapi?”
“Kwa kweli mpaka leo,sijafahamu walipo”
“Walikuwa wana umri gani?”
“Ni wadogo sana”
“Hali hii ilianza lini?”
“Ni miaka mingi sana,baadaye ndiyo akapotea kabisa.Tukawa tunamtafuta kwa kipindi kirefu.Wiki iliyopita tukampata Korogwe”
“Mlivyompata alikuwa katika hali gani?”
“Sijui nikuelezeeje Dokta, lakini bado aliendelea kuwataja watoto”
“Well…Mmesema jina lake anaitwa nani?”
“Marietha”
“Marietha nani?”
“Marietha Karekezi”
“Ameolewa?”
“Huyo, ndiye mme wake?”
Dokta,akamwangalia Deo kwa macho ya masikitiko makubwa sana!Kama mwanamme mwenzake, alielewa ni machungu gani anapitia.
“Pole sana Mr.Deo”
“Nishapoa”
“Ukionesha ushirikiano,hili tatizo linaenda kuisha.Hao watoto unawafahamu?”
“Ndio,ni watoto wangu”
Ki ukweli,mtoto mmoja ndiye alikuwa wake lakini alisema hivyo ili kuepuka mahojiano mengine zaidi.
“Wako wapi?”
“Kwa kweli sijui,sababu kuna kipindi tulipoteana.Kutokana na maisha ya hapa na pale.Baada ya miaka Fulani ndiyo nikamkuta katika hali kama hiyo”
Deo,akajieleza kwa ufupi ili kuzuia maswali mengine ambayo aliamini dokta angemuuliza.
“Nitajua cha kufanya,nitakapofikia nitakwambia.Lakini inabidi sasa hivi awe chini ya uangalizi maalum”
“Atapona?”
Deo akauliza kama mtu aliyekata tamaa na matumaini.
“Tuombe Mungu”
Jibu hilo lilikuwa tata,Deo akageuka na kumtizama Mke wake Marietha aliyekuwa kitandani,kimya amefumbua macho yake lakini hasemi kitu chochote kile.Bado katika macho yake, alikuwa mrembo na alimuona bado mpya, hiyo ilitokana na chembechembe za mapenzi alizokuwa nazo bado, ndani ya damu yake!
“Dokta,nakuomba”
Akamgeukia tena daktari.
“Nitajitahidi”
Jibu la Dokta Makalla, bado liliendelea kuwa tata,hapo hawakukaa sana,wakaruhusiwa lakini Deo alisogea mpaka karibu na kitanda alicholala Marietha,akainama kidogo na kumpiga busu juu ya paji la uso.
“Nakupenda mke wangu”
Deo,akasema kwa uchungu! Huruma ikiwa imemjaa.Jambo hilo lilimfanya Vaileth, azidi kuduwaa,hata siku moja kwake hakuwahi kufikiria kama duniani kuna wanaume kama Deo,kwa historia ya Marietha na mambo aliyofanya aliamini kwamba hakustahili kuwa na mwanamme kama Deo,mstaarabu na mwenye mapenzi ambayo hata shetani aliyaogopa.
“Shemeji”
Vaileth,akaita alivyomuangalia Deo machoni, akamuona kama ni mtu aliyekuwa analengwa na machozi.
“Naam”
“Atapona tu,Mungu wetu ni mwema”
“Tuamini hivyo”
Marietha,akaachwa hospitalini.
********
Jukumu la kurudisha akili za Marietha, likahamia mikononi mwa Dokta Filbelt Makalla, bingwa aliyebobea na kucheza na akili za binadamu wenzake.Siku hiyo, ilivyofika jioni Dokta Makalla akamchukuwa Marietha na kumpeleka ofisi yake nyingine kwani mbali na kuajiriwa hapo TMJ, alikuwa ni dokta wa saikolojia, aliyefungua ofisi yake Mikocheni kwa Warioba,hapo Marietha alikabidhiwa kwa daktari mwingine aliyeitwa Shafik!Kazi ikaanza mara moja kwani Marietha kufika na kufika, akawekwa ndani ya chumba kikubwa ambacho hakikuwa na kitu chochote kile ndani yake,isipokuwa kioo kikubwa ambacho Dokta Makalla na Shafik, walikitumia kumuangalia,hapo walisubiri mpaka nguvu ya dawa alizochomwa ziishe ili waone ni kitu gani atakifanya,baada ya masaa mawili kukatika.Marietha,akarudiwa na fahamu zake.Akaanza kutizama huku na kule!Hapo Dokta Makalla na Mwenzake Shafik,wakawa makini kuliko kawaida.
“Dawa zimeisha nguvu,subiri tuone”
Madaktari hawa,wakasemezana!Marietha alikuwa yupo katikati ya chumba hiko,akaanza kushangaa shangaa kama msukule aliyetolewa kuzimu na Mchungaji Gwajima!Marietha,akasimama taratibu na kuanza kutembea huku na kule, akishangaa shangaa,mara aangalie kule mara huku.Alivyoona kioo akatulia.
“Wewe nani tena?”
Marietha,akawa anaongea na kioo.Jambo hilo walikuwa wakilisubiri madaktari.Hapo ndipo wangejua,tatizo la Marietha kwani kila alichokuwa anakisema madaktari walikisikia.
“Nakuuliza wewe ni nani,lakini umefanana namimi.Ha! Haa! Haaaaaa…Newewe unacheka,Wewe! Wewe! Wewe!”
Marietha,akazidi kuzungumza.Kila kitendo akikifanya, alimuona mtu kwenye kioo nayeye anamuiga.Kwa akili yake alidhani wenda ni mtu,kumbe ni yeye mwenyewe!
“Alafu nipe Abraham, Wiliam uko wapi Mwanangu?Hapa yaani kuulee Mwalimu Nyerere amekutana na Nkwane Nkurumah,Kariakoo Mabibo”
Marietha,akaanza kuchanganya Mafaili,akili yake ilikuwa imevurugika.Mbali na hapo madaktari hawa kuna kitu walijifunza na walijua wapi wangeanzia.
Dokta Makalla,akafungua mlango,akazama ndani.
“Abraham,ndiye mimi nimekuja”
Dokta Makalla akaongea huku akimtizama Marietha.
“Nenda toka hapa,chavi chavi wewe dudu washa.Nenda hapa,unauza nini?Abraham gani?Wewe sio Abraham”
“Mimi ndio Abraham Mama”
“Toka hapa,chizi nini wewe.Embu nitokee”
Dokta Makalla hakuogopa,akazidi kusogea karibu zaidi.Marietha akaonekana kuogopa na kuanza kurudi nyuma.
“Marietha,usiogope.Usiogope simama”
“Mwizi wewe,unataka kuniiba.Abraham wangu na William nawataka wamekufaa”
“Nisubiri hapo,nakuja kukwambia”
Marietha,akawa anakimbia huku na kule kama mtoto mdogo aliyekuwa anacheza kidali poo!Mwisho,akatulia kwenye moja ya kona na kukaa chini,akaanza kulia kwa sauti huku akitaja majina ya watoto wake,hapo ndipo Dokta Makalla, akasogea karibu,nayeye akakaa chini.
“Abraham ndio Mimi,Wiliam anakuja”
“Paaaaaaaa!”
Kilikuwa kibao cha nguvu,kilichotua juu ya shavu la Dokta Makalla na kutoa kelele,sio siri kilimuingia na kumtia hasira lakini ilibidi atulie sababu alielewa aina ya binadamu, anayezungumza naye.Akarudi nyuma kidogo sababu aliogopa kupokea kibao kingine!
Mbali na Marietha kuwa mkorofi lakini ndani ya dakika tano,akawa ametulia kama maji mtungini,Dokta Shafik aliyekuwa nje hakutaka kuamini kitendo hiko,akabaki kwenye kioo, kutizama sinema hiyo.
“Abraham na Wiliam,Abraham na Wiliam.Nikuletee uwaone?”
Dokta Makalla,akawa anafanya kazi, akimtajia majina ya watoto hao,ambayo yakamfanya Marietha atulie abaki akimwangalia tu,hiyo ikawa hatua ya kwanza ya milango mingine kufunguka.
Zoezi la kurudisha akili za Marietha halikufanywa na madaktari wawili tu,bali Dokta Filibert Makalla aliwapa kolabo madaktari wengine saba kwani kazi hiyo ilionekana kuwa ngumu kidogo!
“Siku zote, kidole kimoja hakiweza kuvunja chawa”
Huo ndio msamiati aliokuwa anautumia Dokta Makalla kila kukicha,akiamini ya kwamba umoja siku zote ni nguvu!
***********

Siku zilikatika, hatimaye mwezi ukaisha,bado akili za Marietha zilikuwa zina matatizo,Deo hakuacha kupiga simu kila siku kuulizia hali ya mkewe na wakati mwingine alikata tamaa kabisa!
“Niambie ukweli Dokta,mke wangu atapona?”
Deo,akauliza simuni akionesha kama mtu aliyekata tamaa kabisa!
“Tunajitahidi”
“Lakini hilo sio jibu”
“Nitapambana kwa nguvu zangu zote”
“Bado hujanijibu Dokta,sisi ni wanaume.Niambie kama hatoweza kupona ili nifanye taratibu nyingine”
“Ikishindikana nitakwambia”
“Sawa”
Deo akawa amepoteza matumaini,licha ya yote hakutaka kukubali ya kwamba ipo siku moja atakuja kuishi na Marietha kama zamani,aliamini ya kwamba siku moja Marietha atapelekwa milembe akakae na watu waliokuwa na akili kama zake,mbali na kuwaza hayo hakutaka mambo yafike huko ndiyo maana alijaribu kuulizia ulizia madaktari wengine!
Katika harakati zake za kumtuliza Marietha, huku nyuma alikuwa ana michakato mingine,alikuwa tayari amenunua kiwanja na anajenga nyumba za kuishi wanafunzi yaani ‘Hostels’na wakati huohuo alikuwa tayari yupo katika makubaliano ya kununua nyumba, iliyokuwa jijiji Dar es salaam,maeneo ya Upanga!Ilikuwa kama bahati kwake kwani familia iliyotaka kumuuzia nyumba walikuwa wanasafiri kwenda kuhamishia makazi yao,nchini Germany.
“Nyumba ndiyoo hii.Ina vyumba nane…Huku ni jikoni….Njoo huku kuna toilet….Huku ni uwani,nilitaka nitengeneze Swiming pool.Unaona nilikuwa tayari nishaanza kupima lakini pia kuna vyumba vya nje.Unaweza ukaweka wapangaji…Oh My God,sijakuonesha parking ya magari pia”
Mzee aliyekuwa anamzungusha Deo,kwa harakaharaka kwenye umri walifananafanana,lakini mzee huyu alionekama ni mzee zaidi kwani kichwa chake kizima kilijaa nywele nyeupe yaani mvi.
Alikuwa akimzungusha Deo kila sehemu,ilikuwa ni nyumba kubwa naya kisasa sana.Kwa Deo nyumba kama hiyo na bei aliyotaka kuuziwa ilikuwa ni sawa na zali ya mentali.
“Nyumba nimeipenda.Ni kubwa na nzuri.Nitainunua,unategemea kuondoka lini?”
“Within this week,mke wangu na watoto watatangulia. Mimi after one month ndio nitaenda,unakunywa wine?”
“Natumia lakini sasa hivi,niko sawa”
Deo alivyomalizana na Mzee huyo,akanyooka moja kwa moja kwenye akaunti zake zote!
Akili yake ikafanya kazi kwa kasi kama kompyuta isiyokuwa na mafaili,akapiga hesabu zake za harakaharaka.
“Hapa nikitoa pesa hizi,nitayumba.Inabidi nikachukuwe mkopo benki.Zile Hostel ndiyo zitarudisha pesa za mkopo”
Mwanamme huyu alipiga mahesabu marefu mno na aliangalia mbele umbali wa kama maili elfu nane hivi.
“Inabidi nikope pesa nyingi na hizohizo zitamaliza hostels”
Alizungumza mwenyewe na kuingia ndani ya gari.Ni kweli,wazo lake alilifanyia kazi lakini kabla ya yote alimuibukia Mtui na kumchana kila kitu kilivyokwenda!
“Kama una ndoto ya kuwa mfanyabiashara mkubwa,usiogope mkopo.Kama ukiogopa mkopo sahau kuwa mfanyabiashara mkubwa.Unaikumbuka hii sentensi yako Deo?Ulikuwa ukiniambia maneno haya?”
Mtui,alisema na kuuliza swali.
“Lakini sasa hivi na umri huu,mikopo tena.Naogopa sana”
“Deo,wewe ndiye uliyenifundisha na kunipa ujasiri.Mpaka leo ndio njia zangu,nikikwama naenda benki kukopa.Japokuwa kuna kipindi kidogo mali zangu zipigwe mnada”
“Kwanini?”
“Nilikopa benki kwa niya kununua shamba la mpunga Mbeya kule”
“Ikawaje?”
“Matokeo yake,nilivyopata ile pesa.Nikaenda kununua hisa za Vodacom”
“Hapo ndio ulikosea ndugu,wengi wanakosea sehemu ndogo.Ukikopa mkopo benki,kama una niya ya kujenga nyumba nenda kajenge yaani usitoe hata shilingi moja!Maliza hiyo nyumba yaani hata kama una niya ya kununua sahani ukiona kijiko usinunue tafuta sahani mpaka uipate,kuna wengine wanakopa benki mara akipata pesa anabadili mawazo anaenda kununua gari,lazima uyumbe”
“Hilo nalo neno.Naona tushakuwa wahenga sasa”
“Ha! Haa! Haaa! Haaaaa!”
“Vipi Abraham,ulimpata?”
“Bado,lakini nishajua pa kuanzia”
Siku hiyo Deo na Mtui walipiga stori kama kawaida yao usiku wakiwa nje kwenye gadeni na glasi za mvinyo,waliongea vitu vingi hususani vitu vya maendeleo!Deo hakutaka wazo lake libaki kichwani,mwanamme huyu alikuwa mtekelezaji na sio mvivu, linapokuja swala la kupiga hatua katika maisha,mchakato wa kuandika barua ya mkopo ukaanza mara moja,akafanikiwa kumpata msichana mmoja mrembo aliyeitwa Sara Sanga!
Kutoka katika benki ya Acess,ikatakiwa apeleke kila kitu,kuanzia hati ya mashamba yake pamoja na kiwanja alichonunua.
“Hii tunataka original yake pamoja na passport size mbili.Alafu barua ya serikali za mitaa mbona sijaona hapa?Pia anahitajika mdhamini wako.Mkeo ama watoto wako wasaini hapo kama hawapo,mtu wako wa karibu.Ajaze hii fomu,aandike na akaunti namba zake za benki”
Sara Sanga,alimpa maelekezo mteja wake!Deo alikuwa makini kusikiliza kila kitu,mkononi akiwa na hati zote za vitu anavyomiliki mpaka Fuso zake mbili,kichwani alikuwa mwenye hofu kwani kitendo cha kushindwa kulipa deni hilo aliloenda kukopa la milioni mia tatu hamsini,ingemaanisha mali zake zote kufilisiwa,alivyowaza hivyo ilikuwa kidogo aghaili.

Siku tatu baadaye akawa amekabidhi kila kitu,kilichokuwa kinasubiriwa ni uchunguzi wa kina ufanyike ili benki ihakikishe kama mali za Deo ni kweli anamiliki yeye kwani waliogopa utapeli na kupigwa changa la macho!
Kila kitu kilivyokuwa sawa,mkopo ukatoka.
Deo hakuchelewa,haraka akaenda kununua nyumba ya kisasa, ambayo aliambiwa inauzwa.Hiyo ikawa furaha kubwa sana kwake kwani tayari alikuwa ana miliki nyumba yake mwenyewe kwa mara nyingine.Mtui nayeye alikuwa naye bega kwa bega,wote wakiwa wenye furaha.
“Basi hapo Deo,najua utanisusa sana.Kwangu utakuwa huji tena”
“Bwana Mtui,nani kasema?Pale pia ni kwangu.Hapa ni kwako pia.Mimi ni ndugu yako”
“Sio,siri.Hii nyumba ni nzuri na kubwa mno.Bwana wee!Hii seble kama ukumbi.Hapa unaweza ukafunga goli moja kule na lingine huku watu wakacheza mpira”
Mtui,akamwaga sifa za nyumba hiyo kubwa.Akampa mkono wa hongera Deo Karekezi huku wakiendelea kuzunguka na kuangalia Mandhari ya nyumba hiyo.Kwa Deo, ilikuwa hatua nyingine kubwa katika maisha yake.
“Nina amini bila kupata matatizo kipindi cha nyuma,ningekuwa mbali sana”
“Hapana Deo,kila kitu kina sababu yake.Mungu,ana makusudi yake kufanya vile.Chukulia kama changamoto.Maisha ni kama safari,pamoja na mambo yote yatakayotokea katikati ya safari lakini ni lazima ufike ulipokusudia kufika”
“Ni kweli kabisa”
Huo,ndio ulikuwa ukweli halisi ya kwamba Deo Karekezi maisha yake, yalianza kurudi kwenye mstari tena upya! Jambo ambalo hakutaka kuliamini katika maisha yake!
Siku zilizidi kwenda mbele akiwa anampiga simu hospitalini kila siku kuulizia hali ya Marietha,baada ya miezi mitano kupita.Akapigiwa simu siku hiyo,iliyomshtua na kufanya mapigo yake ya moyo yabadilike!
“Kuna nini dokta?”
“Nina surprise yako.Ebu njoo”
“Dokta…Ku.”
“Mr.Deo…Njoo ofisini kwangu bwana,mbona una mushkeli mzee”
“Wapi?”
“Kwa warioba”
“Sawa nakuja”
Deo alikuwa nyumbani kwake siku hiyo,ndani ya jumba lake jipya,akatoka nje na kufunga na funguo mlango kwani alikuwa bado akiishi mwenyewe,akatembea mpaka getini na kulisukuma!Akatoa gari nje na kurudi karibu na geti tena,akalifunga!Safari ya kwenda kwa dokta Filbert Makalla ikaanza mara moja,dakika arobaini na tano baadaye, akawa amefika na kuambiwa aingie ndani.
“Dokta,kuna nini?”Deo,akaibuka na swali kabla ya kukaa kitini.
Lakini Dokta Filbert Makalla,akamkaribisha na tabasamu.Hiyo ilimaanisha kuna habari njema mno!
“Kaa chini”
“Marietha yuko wapi?Amepona?”
“Nisubiri hapo”
Dokta Filbert Makalla,akainuka na kutoka nje.Dakika moja baadaye,mlango ukafunguka!Akaibuka Dokta Makalla,nyuma akiwa na Marietha.Deo,alivyomuona kwanza hakuamini, pili alisimama wima kama mlingoti, tena bila kupenda!
“Deo!”
Marietha,akaita!Mapigo ya moyo ya Deo yakapiga kwa nguvu!
“Mariethaaaaa……”
Kwa kasi ya ajabu Marietha,akatembea mpaka kwa Deo,akamkumbatia kwa nguvu zote huku akimwaga machozi na kulia kwa sauti.
“Na..omnba nisa..mehe Deo M..me wangu”
“Nimekusamehee MKE WANGU”
Deo,alizungumza kwa kujikaza lakini ghafla nayeye akahisi mashavu yake yanalowana,ni wazi kwamba alikuwa ana uchungu kupita kiasi ndio maana akashindwa kujikaza akaanza kulia,kila kilichotokea kilikuwa ni kama ndoto na muujiza mkubwa sana,akili za Marietha kurudi!
“Abraham na Wili..am wameku..fa”
“Hawaja..fa mke wangu.Wapo hai”




Wiliam hakukoma,aliendelea kumlia misele Karishma kila siku iendayo kwa Mungu,akijaribu kutumia mbinu tofauti tofauti lakini hakuweza kumpata Karishma,akajaribu kutega mitego yake mbalimbali lakini hola,kilichomuumiza zaidi hakuona dalili yoyote ile ya Karishma kumkubalia.Jambo hilo, lilimuumiza sana akili yake kwani katika maisha yake hakujua kitu kupigwa kibuti na mtoto wa kike,yeye alizoea kutongoza mara moja tu na kukubaliwa ama kutongozwa lakini kwa Karishma ilikuwa kinyume chake, kwani ulikatika mwezi mmoja na nusu bila ya kuambulia hata kumshika mkono Karishma,zawadi zake mbalimbali alizopeleka na maua vilikataliwa kabisa,mara akaingia kwa gia ya pesa nayo haikufua dafu hata kidogo, jambo hilo lilimuumiza sana akili,moyo ulimuuma ajabu.Rafiki mkubwa wa Karishma siku zote aliitwa Adamma Chuku Emmeka,huyu alikuwa ni msichana kutoka Nigeria,walitokea kuwa marafiki wakubwa sababu ya msichana huyu kutoka Nigeria kuwa Siriazi katika masomo,hakuwa msichana mwenye mambo mengi kama wengine chuoni hapo,hiyo ilifanya kuona ya kwamba Adamma Chuku Emmeka ndiye atakuwa rafiki yake wa karibu.
Ni kweli, marafiki hawa tabia zao zilifanana kabisa kwani wao hawakuwa na makuu,kwao ulikuwa ni mwendo wa kitabu na darasani tu!Hawakuwahi kuonekana hata siku moja kumbi za Starehe,kilichokuwa kinamfurahisha sana Karishma ni kugundua pia Adamma ni msichana anayependa kusali yaani mchamungu,walikuwa wakitembea pamoja kila kukicha,kama Adamma yupo kulia basi Karishma kushoto!Jambo hilo likafanya wazushiwe skendo mbaya ya kuwa wanasagana,habari hizo zikasambaa kwa kasi ya moshi wa kifuu.Chuo kizima cha Stockholm wakaamini kwamba Adamma na Karishma ni mtu na mpenzi wake,hilo halikuwa tatizo kwa nchi za Ulaya, kwao ilikuwa ni kitu cha kawaida kabisa!
“Kwahiyo Yule demu,anasagana kumbe.Adamma ndiyo anamsaga?”
Habari hizo zilivyomfikia Wiliam,akapandisha mori!Akauliza kwa jazba huku akitetemeka kwa hasira kutokana na wivu aliokuwa nao!Haikuwezekana hata kidogo, jambo hilo kuliacha hivihivi.
“Ndio kaka,wale mademu wanasagana”
“Unasema ukweli?”
“Sina utani nawewe Raphael”
“Adamma,atanitambua”
Dakika hiyohiyo Wiliam akasimama wima huku akiwa ameukunja mdomo wake kwa hasira,picha ya Addama ikamjia kichwani,hakuelewa amfanye nini msichana huyu muharibifu.Ilikuwa ni siku ya Jumamosi,siku ambayo wanafunzi hupumzika kwenye vyumba vyao,na wengine walilazimika kufua nguo zao siku hiyohiyo!Wiliam, alikuwa akipishana na watu kwenye ngazi,wengine aliwapiga vikumbo bila kujali,hasira za kijana huyu zilikuwa chafu na chuo kizima kilimtambua, ndio maana hata wanafunzi wenzake walimuogopa!
“Addama yuko wapi?”
Wiliam aliuliza kwa jazba baada ya kumkuta mwanafunzi wa kizungu anashuka ngazi.
“Yuko huko chini,anafua”
“Wapi?”
“Nyuma huku”
Wiliam badala ya kupanda ngazi,akaanza kushusha.Staili aliyokuwa anashuka nayo ilitisha kwani aliruka ngazi tatu tatu,alivyoufikia mlango alikunja kona kama gari lililokatika breki,kwa mbali alimuona Addama,anafua nguo zake,akamfuata kwa kasi!
“Wewe msagaji”
Wiliam alivyofika,akashika nywele za Adamma zilizokuwa ndefu,akamuinua hivyohivyo bila kujali maumivu anayohisi.
“Rap..hael unaniumiza,niache”
“Siwezi kukuacha,lazima uniambie.Vinginevyo leo hapa,nitakinyofoa kichwa chako”
“Nini lakini?”
“Kwanini unamsaga Karishma?”
Wiliam,akaibuka na swali,Macho yake yalikuwa mekundu kupita kiasi,kulikua kuna kila dalili mbaya ya ugomvi siku hiyo endapo Adamma angejibu, shombo!
“Sijawahi kumsaga,ni rafiki yangu tu”
“Sio kweli”
“Kama huniamini basi”
“Alafu usinijibu hivyo.Najua unajua navyompenda”
“Naelewa Raphael”
“Sasa kama unataka kuishi kwa amani hapa chuoni,fanya unavyojuwa Karishma awe mpenzi wangu”
“Lakini sidhani kama atakubali”
“Kama asipokubali hilo ni swala lako, sio langu”
“Sawa,nitamueleza”
Kichwa cha Adamma siku hiyo kiliuma ajabu, kutokana na nywele zake kuvutwa na mvulana huyu mshenzi anayelazimisha mapenzi,habari hizo akamfikishia Karishma,hapo ndipo moto ulipowaka.Katika siku ambayo Karishma alitibuka ni siku hiyo!Hakuwahi kukasirika kama siku hiyo,ndiyo maana alikuwa anavaa nguo zake harakaharaka ili akamuibukie Wiliam ampe vidonge vyake,kitendo cha Adamma kuteswa kilimuuma ajabu!
“Lakini Karishma achana naye tu.Mvuta bangi Yule”
Adamma,akajifanya kumkingia Wiliam kifua.Alijua nini maana yake endapo Karishma akienda kumtukana Wiliam.
“Wacha nimfate,naomba huo mtandio wangu hapo mezani”
“Msamehee tu”
“Siku nyingi sana,nimemkalia kimya.Wacha nikamtolee uvivu leo”
Alichotaka kukifanya ndicho kilichoenda kutokea,baada ya kuvaa kila kitu.Akajifunga mtandio kichwani,akatoka nje mbiombio na kuanza kumuulizia Wiliam alipo.
“Kaingia chumbani kwake sasa hivi”
Mwanafunzi mmoja akamjibu Karishma!
“Kwake ni wapi?”
“Chumba namba 25B”
“Ahsante”
Moyo wa Karishma ulijawa na hasira mno,akatembea na kukatiza mabweni,akaibukia mlangoni kwa Wiliam,akagonga!Mlango ukafunguliwa,kitendo cha Wiliam kumuona Karishma,moyo wake ukapiga sambasoti, akajua tayari amekubaliwa na mtoto ameanza kujaa kingi.
“Karibu ndani kisura,nimefurahi umekuja leo!Adamma amekupa ujumbe wangu?”
Wiliam akaanza kujieleza mwenyewe, kabla hata ya kuulizwa kitu.
“Nisikilize kwa makini Raphael.Hata utumie mbinu gani, siwezi kuwa nawewe hilo moja alafu cha pili,unikome popote utakaponiona pita mbali na usiniongeleshe hata kidogo!Kingine kwa kukuhakikishia kama siwezi kuwa nawewe,hata wanaume wote wafe duniani ubaki peke yako sitoweza kukupenda!Na ukome kusema mimi ni mpenzi wako,nikisikia tena.Utaimba haleluya”
Karishma alizungumza kwa sauti ya juu,akiwa mwenye jazba kwa kiasi cha kutosha, hiyo ilimfanya Wiliam aishiwe pozi,akashindwa kujibu sababu ya watu waliokuwa wanapita kwenye korido.
“Karshma ni…”
“Achana na mimi,unikome.Mbwa wewe”
Karishma,akamwaga matusi.Alivyohisi hasira zake zimeisha, akageuza na kuondoka zake! Hiyo, haikufanya Wiliam,asitishe kumuwinda,alipiga moyo konde na kuendelea kumgasi tena, alimsumbua na wakati mwingine alidiriki kusimama mbele za watu wengi na kutamka ‘Nakupenda Karishma’wengi wakajua tayari Wiliam anaanza kuwa chizi mapenzi.
Siku moja darasani,aliwaacha watu vinywa wazi, baada ya kuibukia darasa analosoma Karishma.
“Samahani mwalimu”
Alimuomba mwalimu ruksa,baada ya kumkuta anafundisha mbele!Kila mtu akamwangalia yeye.
“Unasemaje Rapahel”
“Kuna mwanafunzi ninampenda sana humu darasani kwako.Naomba nimtaje”
Kitendo cha kusema hivyo, kilimshangaza mwalimu na kila mwanafunzi aliyekuwa ndani ya darasa,kila msichana alitega sikio lake akidhani wenda ndiyo wanaenda kutajwa na kila mtu alikuwa na shauku isipokuwa mrembo huyu Karishma aliyekuwa, anafahamu kila kitu.
“Anaitwa Karishma nampenda sana huyu mrembo!Nipo radhi kufanya chochote juu yake.Nakupenda Karishma,tafadhali nikubalie”
Wiliam alizungumza huku akimuangalia Karishma,hakuna mtu aliyekuwa tayari kuamini kama Wiliam, angeongea kinyonge na hisia namna hiyo,kila mtu akamgeukia Karishma kumuangalia ni kitu gani angejibu lakini matokeo yake,hakuonesha ushirikiano hata kidogo na wala hakuwa na habari,hiyo ilimaanisha kwamba hayupo tayari.

***********
Iliaminika kwamba chuoni hapo Karishma hana mahusiano ya aina yoyote ile,skendo ya yeye kusagana na Adamma ilimsumbua kupita kiasi na kumkosesha raha,ilikuwa ni lazima apambane na hali hiyo.Kichwa kilimuuma kila kukicha lakini pia,akapata wazo moja tu!Siku moja, alimtafuta mwanafunzi anayeitwa Harry Cage,mwanafunzi aliyekuwa anasoma sheria mwaka wa nne.Kuna jambo alitaka kuzungumza naye, ndiyo maana akamuita kwenye mgahawa siku hiyo.
“Nataka ujifanye wewe ni mpenzi wangu”
Karishma baada ya mazungumzo hayo,akasema shida yake!
“Kivipi?”
“Tuigize mimi nawewe ni mtu na mpenzi wake”
“Lingine?”
“Hilo tu,lakini nitakuwa nakulipa”
“Hakuna shaka,umendaa kiasi gani cha pesa?”
“Dolla kumi kwa siku”
“Poa”
Swala hilo likawa tayari limesukwa,kitu alichotaka kukifanya Karishma kilifanyika kwani baada ya wiki tatu mbele kufika,habari zilitapakaa chuo kizima kwamba Harry anatoka na Karishma kimapenzi.Hiyo ilikuwa wazi kabisa kwani walikuwa wakionekana pamoja na mara nyingine Harry alikuwa akimshika kiuno Karishma mbele za watu,hakuna hata mmoja kati yao aliyekuwa anajua kwamba walikuwa wakiigiza.Habari hizo zilivyomfikia Wiliam,akaja juu kwa hasira,akaingia ndani kwake na kuvuta friji,akachukuwa mzinga mkubwa wa wisky akaumimina mdomoni,alivyoutoa ukawa upo nusu!Akashusha pumzi na kutoka nje,kabla ya kupiga hatua nne simu ikaita,haraka akaipokea na kuiweka sikioni.
“Sema shidaa yako haraka haraka”
“Raphael mpenzi,upo sawa?”
Sauti hiyo ilikuwa ya Vivian,mwanamke wa kimarekani mtoto wa kishua, ambaye alikuwa ana mahusiano naye!
“Ndio”
“Lakini siku hizi mbona umebadilika?”
“Nimekuwaje wa kijani kibichi?”
“Sikuelewi mpenzi wangu,hunipigii simu kama zamani”
“Kama hunielewi basi”
“Unasema nini Raphael?”
“Kama ulivyonisikia,naomba usiwe unanipigia simu tena, kuniuliza upuuzi na ujinga”
“Raphael Rapahel… tititiii”
Hapohapo Wiliam akakata simu na kuutafuta mgawaha ambao aliambiwa kwamba Karishma na Harry wapo hapo,akafika moja kwa moja, meza ya mwisho waliyokaa wanakunywa juisi,akavuta kiti nayeye akakaa pembeni yao huku akimtizama Harry kwa macho makali.
“Kidume,Harry!Kwahiyo umeamua kunichukulia demu wangu…Sio?”
Wiliam akauliza.
“Harry,naongea nawewe”
“Raphael naomba utupishe,nishakwambia sikutaki”Karishma akaingilia kati.
“Siongei nawewe Karishma,nyamaza.Harry nijibu”
“Sio hivyo mshka…”
Harry hakuweza kumalizia sentensi yake,Wiliam akawa keshanyanyua glasi ya juisi na kuimimina kichwani yote!Jambo hilo Harry akalitafsiri kama dharau hakutaka kulifumbia macho,kwa kasi ya mwewe akavuta kiti kwa nyuma na kumuinua Wiliam,akamtandika ngumi ya tumbo,Wiliam nayeye hakukubali, akatupa ngumi iliyomfikia Harry mdomoni,akampiga na kifuti cha tumbo,ndani ya sekunde tano mgahawa ukawa umevurugika.Harry na Wiliam wakajaza watu,walikuwa wakipigana na kutupana huku na kule!
“Rapaheeel,Raphaeeel”
Karishma alijaribu kutuliza ugomvi huo lakini Raphael, alionekana ndiyo kwanza kama ameanza kwani alizidi kumpiga misumbwi ya usoni na puani,akamkwinda shati Harry na kumpiga kichwa cha pua!Ugomvi, ulikuwa mkubwa kiasi kwamba walimu wakaingilia kati na kuwaachanisha.

*********

Penzi la Abraham na Mama Maria,lilipamba moto siyo kitoto!Wakati mwingine Mama Maria alijisahau kabisa, akawa anamnyonya mdomo Abraham waziwazi wakiwa kwenye migahawa, tena mbele za watu.Kila siku Abraham kwake alionekana mpya,sio kitandani tu hata jinsi alivyokuwa mtanashati,mbali na hapo mama huyu alijuwa kumgharamia,akawa anamnunulia nguo nzuri kila wakiwa pamoja!Kifupi, Abraham alizidi kung’ara, kila msichana aliyemuona alitamani kuwa naye,hata kama ungekuwa mke wa nani ilikuwa ni lazima umtamani Abraham,sababu alikuwa ana uzuri wake wa kipekee.Kitu kilichokuwa kinamfurahisha Mama Maria ni kutokana na Abraham kuwa na misimamo,hakuwa mvulana wa kujirahisisha.Wachache walibahatika kupata nafasi ya kuongea naye!Habari za Abraham kusafirishwa Mwanza kwenda kuanzishwa shule nyingine, zilivyomfikia Mama Maria,siku hiyohiyo akaenda Mwalimu Nyerere na kupanda ndege.
Kitendo cha Abraham kufika na basi,akamkuta Mama Maria anamsubiri tayari jijini Mwanza,hapo wakaongozana mpaka hoteli inayoitwa Midland.
Damu ya Mama Maria, ilikuwa inaenda kasi sio mchezo, ndiyo maana walivyokabidhiwa chumba na kuingia ndani,akamfakamia Abraham mdomoni, wakaanza kubadilishana mate kwa njia ya kunyonyana ndimi,hiyo haikutosha, wakaanza kusukumizana, Abraham akatupwa kitandani,puu chali.Mama Maria akapanda kwa juu,akaanza kuchomoa mkanda wa Abraham kwa fujo sana,akashika suruali na boxa akavivuta kwa pamoja.Moto aliokuwa nao,haukuwa wa kawaida, ndiyo maana baada ya kuona ndizi ya Abraham tayari imesimama,akateremsha chupi yake na kupandisha shati juu,akaipanua miguu yake huku na kule,akakalia ndizi ya Abraham,mambo yakaanza hapohapo!

********
Ugomvi,alioanzisha Wiliam siku hiyo kwenye mgahawa,ulifanya ufike katika uongozi wa chuo anachosoma,hakukuwa na mjadala wowote ule.Kutokana na jina lake kuwa katika’ black book’yaani kitabu cha watoto watukutu,ilibidi asimamishwe chuo kwa muhula mmoja mzima.Alivyojaribu kuomba msamahaa,ikashindikana kwani barua ilichapwa Wiliam akawa amesimamishwa chuo!
“Nimesimamishwa chuo kwa ajili yako Karishma,nakupenda.Sitoacha kukupigania!Nitakupigania mpaka utakaponikubalia,tutaonana muhula ujao, Mungu akipenda”
Katika siku ambazo aliongea kwa uchungu ni hiyo,Wiliam alimwambia Karishma jinsi anavyoumia na baada ya kuongea hivyo,akaondoka zake akimuacha huku nyuma Karishma anamsindikiza kwa macho,akahisi moyo wake unauma ajabu.Akataka kumsimamisha,lakini akaupiga moyo wake ‘stop’
“Lakini mimi sina kosa lolote”
Alizungumza mwenyewe na kuondoka zake, kuelekea darasani.Kuanzia siku hiyo Karishma alianza kuishi kwa raha,karaha za Wiliam zikawa hazipo tena ingawa wakati mwingine alimkumbuka na alianza kuona sura yake inampitia kichwani.
“Sitaki hii hali itokee,sitaki kumkumbuka”
Karishma hakutaka kumkumbuka Wiliam,akaendelea na masomo yake,wanauwe kwa wazee waliendelea kumsumbua lakini msimamo wake siku zote ulikuwa uleule.Mpaka muula wa kwanza unaisha na kufunga chuo kwa ajili ya likizo hakukuwa na mwanaume yoyote Yule, aliyeweza kumgusa wala kumshawishi,hatimaye Karishma akarejea nyumbani kwao Tanzania,kuanza likizo.
Kitendo cha kutua uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere,moyo wake ulijawa na furaha.Cha kwanza kukiwaza ni wazazi wake,alikuwa ana mengi siku hiyo ya kuwahadithia tangu alivyofika Sweden na masomo yake kwa ujumla,ndiyo maana alikuwa mwenye mushkeli.
“Maaaaaaaaaam”
Karishma alipiga kelele baada ya kumuona Mama yake mzazi nje ya uwanja wa ndege,akamrukia kwa nguvu zote na kuanza kupigana mabusu ya mashavu!
“Karibu mwanangu,karibu nyumbani”
Dokta Katrina alisema huku akiwa mwingi wa furaha.Hilo, lilionekana waziwazi kwani muda wote meno yake, yalikuwa nje!
“Daad yuko wapi?”
Karishma akatupa swali, walivyokuwa wanatembea kuelekea kwenye maegesho ya magari!
“Amesafiri”
“Anajuwa nakuja leo?”
“Ndio”
Wote wakatembea mpaka kwenye gari na safari ya kuanza kwenda nyumbani ikaanza mara moja.
Karishma alifurahi kufika nyumbani na moja kwa moja akaingia bafuni, kujimwagia maji,alivyotoka akapitiliza mezani kwa ajili ya kupata chakula cha usiku,hapo stori zilianza na hata walivyomaliza kula chakula ziliendelea.Karishma, alikuwa mwenye mengi ya kuzungumza!
“Kesho nitasafiri Karishma,lakini ningependa twende wote”
“Utaenda wapi Mama?”
“Mwanza”
“Mwanza?Natamani kwenda Mwanza!Sijawahi kwenda hata siku moja,twende wote”
“Umechoka lakini..”
“Hapana Maaam”
“Sawa,sijui niseme ujiandae.Maana ni kesho usiku.Asubuhi, nitakupigia simu nikiwa ofisini”
“Sawa Mam,good night”
Hapo kila mtu akamuaga mwenzake,wakaingia vyumbani kulala.

**** ******
Ilikuwa ni lazima Dokta Katrina asafiri Mpaka jijini Mwanza siku inayofuata.Ilikuwa ni safari ya dharura na ni lazima akaudhurie kikao cha madaktari.Kila kitu kiliandaliwa na alitakiwa kufikia hotel ya Midland.Ndio maana siku iliyofuatia, asubuhi na mapema akaingia mitandaoni na kuangalia ndege zitakazoruka usiku wa siku hiyo,Mungu akawa upande wake,akapata shirika la ndege la Precision Air!Akakata tiketi mbili yeye na binti yake.Mambo yakaenda harakaharaka na safari ikaandaliwa,saa moja ya usiku wakawa tayari wapo ndani ya ndege wakisubiri ipae angani,Karishma alikuwa mwenye furaha sana sababu hakuwahi kukanyaga jiji hilo na alilisikia namna ambavyo likisifiwa tu.

**** ******
Mguu mmoja wa Mama Maria,ulikuwa umewekwa begani!Midomo yao ilikuwa ikinyonyana,ulimi wa Mama Maria, ulikuwa umemezwa huku nyoka wa Abraham aliyekuwa mkubwa akiwa ndani ya mgodi wake,Mama Maria kazi yake ilikuwa ni kutoa miguno tu,hiyo ilimpelekea mpaka afumbe macho yake.Raha, alizohisi hazikuwa na kipimo chake,ukizingatia ilikuwa ni asubuhi sana ya saa kumi na moja!Baridi, alilokuwa anahisi lilipotea,hiyo ilitokana na kukunjwa vizuri na mtoto huyu Abraham mwenye PHD kitandani,haikuwa hivyo tu.Mama Maria,alipinduliwa na kuambiwa ashike kona ya kitanda,akawa amebinuka kwa nyuma,Abraham akashika kiuno chake kwa mikono miwili,akamtumbukiza nyoka wake taratibu sana!Alivyohakikisha yupo ukingoni,mwendo wa kurudisha kiuno nyuma na kukipeleka mbele ukaanza hapohapo!Haikufahamika kama Mama Maria,anatoa miguno ya raha ama maumivu lakini alikuwa akisikilizia huku akiwa ameyafumba macho yake!Mara ghafla nayeye,akaanza kukinyoga kiuno chake kwa kasi,akageuza shingo yake na kuomba denda,Abraham akajua nini maana yake,hakutaka kumtesa!Akambinua na kumlaza chali,yaani kifo cha mende.Miguu ya Mama maria,ikawa imechanuliwa huku na kule,hazikupita hata sekunde saba.Mama Maria akawa amemaliza na hapohapo Abraham akasawazisha,akatulia juu ya kifua cha Mama Maria!Siku hiyo, walipiga stori za hapa na pale,ilikuwa ni lazima saa tano ya asubuhi Abraham akaripoti shule!Hivyo ndivyo alivyoambiwa na Mzee Chonga!
“Nitakupeleka Abraham,usijali.Nitakuwa nakuja kukuona pia”
“Sawa Mpenzi”
“Lakini,kumbuka nakupenda sana”
“Hata mimi,nashukuru kwa kunipenda namna hiyo”
Abraham na Mama Maria walizungumza kimahaba!

*******
Kitu cha kwanza baada ya kuzinduka usingizini,aliingia kuoga!Kwa kuwa hoteli hiyo ilikuwa ya kisasa,aliwasha maji ya moto na kujimwagia!Baada ya hapo alitoka na kuvaa nguo safi!
“Mama mimi natoka nje kidogo”
“Sasa unatoka unapajua?”
“Si hapo nje tu,kwenye balcony”
“Kuwa makini”
Dokta Katrina alikuwa bado amelala kitanda cha pili yake,Karishma akafungua mlango akiwa ameshika simu yake ya gharama aina ya Ipohne 6 plus,anachat huku anatembea,akaanza kupandisha ngazi kuelekea juu niya yake, akakae kibarazani akapige picha,katika hali ya kushangaza akapigwa kikumbo begani!Simu yake,ikadondoka chini,moyo wake ukapiga kwa nguvu baada ya kuona simu yake imepasuka kioo,akakunja ndita na kumwangalia mtu huyo aliyempiga kikumbo!
“Samahani”
“Samahani, itanisaidia nini?Simu yangu umepasua!Samahani yako,haitonisaidia”
Abraham,alihisi kupagawa baada ya kuona balaa hilo,simu ya gharama ilikuwa chini imepasuka,alivyojaribu kuomba msamaha ilishindikana.
“Hapana kaka,nilipe tu simu yangu.Kama ukishindwa ninunulie mpya”
Karishma,akaweka ngumu huku akimtizama Abraham kwa macho makali.


Mzozo ulioibuka ndani ya korido ya hoteli ya Midland haukuwa wa kitoto,Karishma alimfokea Abraham utadhani ni mtoto mdogo,simu yake ilikuwa imepasuka kioo tena, ilikuwa haina muda mrefu tangu inunuliwe, hilo ndilo lilimkera zaidi.Kwakuwa Abraham alijuwa amefanya kosa hilo, ilibidi awe mdogo tu,akaanza kuomba msamahaa lakini Karishma alizidi kupaza sauti ya juu akitaka simu yake ilipwe la sivyo Abraham anunue simu mpya.Hapo ndipo ikatokea vuta n’kuvute!
“Nitakulipa,nisamehee sikukuona”
“Hukuniona nini, umefanya makusudi”
“Sio makusudi”
“Sawa,lipa simu yangu”
Karishma alichachamaa,aliyefika kutuliza ugomvi huo ni Mama Maria, aliyetoka chumbani na kumkuta Abraham, akifokewa kama mbwa ama mwizi,hiyo ilimuuma sana!Haikuwezekana hata kidogo amuache Karishma salama.
“Wewe binti kuwa na adabu”
Mama Maria,nayeye akapandisha mori!
“Lakini kanipasulia simu yangu”
“Ndio umfokee hivyo?Kwani ameshindwa kukulipa eeh,naongea nawewe”
“Sio hivyo Mama”
“Kumbe nini?Nimekusikia ulivyokuwa unaropoka huko nje.Simu yako shilingi ngapi kwani?”
Mama Maria,akaitizama simu ya Karishma kwa nyodo.
“Shika simu yako,nakupa na pesa ukanunue mpya”
Kitu alichokisema ndicho alichoenda kukifanya,Mama Maria hapohapo akashuka chini na kutoka nje, mpaka kwenye ATM mashine zilizokuwa karibu,akapakua kiasi cha pesa,akarudi chumbani na kuchanganya pesa zilizokuwepo!
Akarudi na kumkabidhi Karishma.
“Nadhani hiyo simu haizidi,milioni tatu.Keep change!”
Kilikuwa ni kitendo kilichomuacha wazi Karishma ambaye hakutegemea kabisa,akatamani kuomba msamahaa sababu kosa lake alilijua lakini moyo wake ukasita.Siku hiyo Karishma akakosa raha kabisa,alijiona ni mkosaji alitamani amuone Abraham wakati huohuo na amuombe msamaha kwa namna alivyokuwa anamdhalilisha vya kutosha,ndiyo maana alivyosimama nje kwenye ‘balcony’ alikuwa akiwaza jinsi,atakavyomfuata!
“Inabidi nikamuombe msamahaa yule kaka,ni mstaarabu sana.Sijui kwanini nimefanya vile”
Karishma alikuwa akiwaza!Wazo, lililomjia kwa wakati huo ni kushuka chini na kusubiri mapokezi ili aonane na Abraham ili aombe msamaha,hakuwa mwenye uhakika kama wazo lake lingezaa matunda ama la,hivyo ndivyo alivyofanya kwani alianza kushuka ngazi,akafika mpaka mapokezi.Akasubiri kwenye makochi makubwa!Macho yake hayakubanduka kwenye korido iliyokuwa inatokea vyumbani.Kila aliyekuwa anatokeza alimwangalia kwa umakini,dakika kumi baadaye Abraham akatokeza.Bila kujishauri akasimama wima na kumuendea kwa kasi.
“Kaka naomba unisamehee”
Karishma,akamwambia Abraham kwa kumaanisha kwani aliongea kwa upole sana!
“Kwani umefanya nini?Si,umeshalipwa simu yako”
“Licha na kulipwa,nisamehee.Ama ngoja nikurudishie pesa zako.Niombee Msamaha kwa Mama yako”
“Usijali,ni vitu vya kawaida tu”
Abraham aliongea kwa upole,vishimo vya mashavuni mwake vikaingia ndani.Utanashati wake,ukaonekana.Mbali na hapo upepo wa kiyoyozi uliokuwa unapuliza ulifanya Marashi yenye harufu nzuri yapite puani mwa Karishma,hiyo ilimfanya asitamani kumaliza mazungumzo na Abraham.
“Ahsante.Lakini unaitwa nani?”
“Abraham”
“Mimi naitwa Karishma”
Karishma bila kuulizwa jina lake,alijikuta anaropoka.Hata hivyo alijishangaa hata yeye kuna hali fulani alikuwa akiisikia ndani ya moyo wake,ambayo haikuwa ya kawaida.
“Ni mwenyeji wa Mwanza?”
“Naishi Dar es salaam”
“Woow,hata mimi naishi hukohuko”
“Basi vizuri”
Abraham,hakuonekana mtu mwenye kushoboka, alizungumza na Karishma kwa kifupi na hakutaka stori nyingine zaidi,hilo ndilo lililomfanya Karishma ashindwe kumfafanua Abraham vizuri sababu haikuwahi kutokea mwanamme ama kijana yoyote aliyewahi kuongea naye alafu wakaishia hivi juu juu bila kumsifia ama kumuomba namba za simu.Abraham hakuonesha shobo ya kitu chochote kile.
“Nina haraka sana”
Abraham alivyosema hivyo,ndiyo ilimuuma kabisa.Akatamani kumshika mkono kumzuia lakini akashindwa.
“Lakini kaka”
Karishma akaita,Abraham akawa amefika mlangoni,akageuka!
“Naweza kupata namba zako za simu?”
“Za nini?”
“Tuwasiliane,tuwe marafiki”
“Marafiki?!”
“Usinifikirie vibaya,marafiki wa kawaida tu”
“Okay,lakini sitopatikana kwa muda kidogo”
“Kwanini?”
“Naendsa shule”
“Hakuna shaka”
Abraham,akatoa namba kisha kuondoka zake, hata bila ya kusema kwaheri huku nyuma akimuacha Karishma anamsindikiza kwa macho.

********
Hakuna mtu aliyekuwa tayari kuamini kama Deo na Marietha wamerudiana kwa mara nyingine,kila mtu aliyesimuliwa historia ya wanandoa hawa alibaki kinywa wazi.Mbali na hapo wanawake walitamani kumuona mwanamme huyo ana fanana vipi sababu,haikuwezekana kwa mwanamme wa kawaida kutoa msamaha kwa mkewe kirahisi namna hiyo.Deo akawa ameudhihirishia ulimwengu kuwa maisha ya ndoa ama mapenzi ni safari ndefu na iliyojaa changamoto nyingi sana!Licha ya yote,hakutaka kushiriki naye tendo lolote lile,alitaka kwanza wakapimwe ugonjwa wa virusi vya Ukimwi.Hapo ndipo Marietha alihisi tumbo linamuuma ingawa alikuwa akisali kimoyomoyo asikutwe na ugonjwa huo hatari ambao hata yeye aliuogopa!
“Usinifikirie vibaya mke wangu,ndiyo maana nataka wote tupime”
“Sawa Mme wangu lakini mfano nikiwa nimeathirika utaendelea kunipenda?”
Marietha akauliza wakiwa tayari hospitali ya Madona,wamekaa juu ya benchi wanamsubiri daktari wa maabara ili wapime ugonjwa huo.
“Ndio,nitakupenda”
“Unasema ukweli Deo?”
“Ndio Mke wangu na uzee huu unadhani nitampenda nani?Kama nilikupigania katika hali yako mpaka leo,sitoshindwa kuishi nawewe mpaka kifo changu”
“Nakupenda mme wangu.Naomba unisamehe kwa yote niliyokufanyia.Najuta sana”
“Yaliyopita si ndwele.TUGANGE YAJAYO”
Deo akajifanya Muhenga,akapigilia msumari kwa msamiati wake ili kudhihirisha ya kuwa wasiangalie nyuma,wasonge mbele!Daktari alivyofika,wakaingia ndani ya chumba maalum na kabla ya kutolewa vipimo walihojiwa maswali mawili matatu.
“Ugonjwa huu wa Ukimwi,sio kifo.Kwahiyo muwe tayari kwa majibu yoyote yale.Wapo waliokuwa na ugonjwa huu lakini mpaka leo wanaishi,Ukimwi sio kifo kama watu wengi wanavyodhani.Ukishakubaliana na hali hiyo,utaishi maisha marefu”
Dokta Gabriel Fred Masue,alikuwa makini kuwapa ushauri na saha Deo na mkewe,hakuishia hapo.
Akawapa mifano mbalimbali ili kwanza awatoe uwoga,na hilo ndilo lilikuwa jukumu lake,baada ya hapo akawatoa damu na kuondoka nazo,akiwahaidi baada ya dakika kumi angekuwa na majibu tayari.Sio Deo aliyetowa wazo hata Marietha, kifupi kila mtu tumbo lake liliunguruma kwa uwoga!Daktari alivyofungua mlango baada ya dakika saba kupita,ndiyo ikawa patashika, ilikuwa kidogo wamzuie daktari asitoe majibu.
“Majibu tayari”
Dokta akasema na kuvuta kiti kwa nyuma,akaketi!Akamtizama kila mtu usoni kwa kitambo kidogo!
“Kama nilivyosema hapo awali,kuwa na Maambukizi ya Ukimwi sio kifo!Majibu yote yametoka naya…”
“Dokta ebu subiri kwanza!Mkojo umenibana”
Deo,akamkatisha daktari.Alihisi mkojo unataka kumpenya!
“Tulia kwanza utaenda,naomba kuwapongeza majibu yameonesha.Wote ni NEGATIVE”
Moyo wa Marietha ukapiga kwa nguvu,hakuelewa huo ni muujiza ama ni kweli kwani idadi ya wanaume ambao aliwahi kulala nao,ilitia fora.Kabla ya kujishauri vizuri akashtukia amevutwa na Mumewe Deo,hapohapo bila aibu wakaanza kunyonyana ndimi kwa furaha zote.
“Nakupenda sana Mke wangu”
“Namimi nakupenda mme wangu”
Hivyo ndivyo ilivyokuwa.

****** *****
Mambo hayakuishia hapo,ilikuwa ni lazima Deo Karekezi afanye kitu kama shukrani.Ndio maana baada ya kufika nyumbani kwake akiwa na mkewe alianza kumtafuta Mama yake mzazi hewani.
“Ndio Mama yangu kipenzi..Njoo Dar es salaam.Panda ndege nitakutumia tiketi,uje na Eveline!Kesho..Ndio ndio mjiandae mje kwa kweli,Mbona mama umeshtuka,kuna kitu nataka kuwaonesha Mama yangu.Tafadhali naomba uje”
Deo alikuwa simuni,pembeni alikuwa amesimama Marietha bado anashangaa huku na kule anaangalia ukubwa wa nyumba ya Deo,bado hakutaka kuamini kwamba Deo amerudi tena kwenye mstari wakati alifirisika,kuna kitu alijifunza ya kwamba.Maisha ni mapambano,simu ilivyokatwa alianza kumuomba Deo msamaha kwa mara nyingine kwani alikumbuka namna ambavyo alimdharau kisa pesa za Maximo!
“Nimekusamehee Mke wangu,huamini kama nimekusamehee”
“Ndio simaini”
“Nifanye nini ili uamini?”
“Hata sijui”
“Ninakupenda sana”
Marietha bado roho ilimuuma,ilikuwa ni wazi kabisa kwa makosa aliyomfanyia Deo!Hakustahili kusamehewa hata na Mungu.
“Umenisamehee kweli?”
Marietha akauliza tena.
“Sogea karibu mke wangu”
Deo akamvuta Mkewe karibu na mdomo wake,wakaanza kunyonyana denda!
“Ndio ninakupenda,kukuhakikishia hili nataka nikufanyie sherehe kubwa ya kukurabisha nyumbani.Kuhusu Abraham tutampata hivi karibuni na Wiliam pia”
Deo hakutania hata kidogo na alikuwa ana uhakika na jambo analotaka kulifanya ndiyo maana alianza kuwapigia simu,ndugu,jamaa na marafiki.Akiwaambia kwamba ana tafrija ndogo wiki moja baadaye.

Siku iliyofuata Mama yake akawa ameingia na ndege ya mchana,akampokea uwanja wa ndege.Moja kwa moja wakanyoosha mpaka nyumbani kwake,ndani ya jumba lake kubwa.
“Karibu nyumbani MAMA”
Deo akamkaribisha Mama yake.
“Hii ni nyumba yako ama ya yule rafiki yako?”
“Ni yangu Mama”
Hata Mama mwenyewe,alistaajabu.Akabaki kuitolea macho nyumba hiyo kubwa,akamfuata mwanaye na kumkumbatia kwa nguvu huku machozi yakimlenga.
“Hongera sana mwanagu.Mungu ni mkubwa!”
“Amen Mama”
Hata mdogo wake Eveline,alibaki akishangaa na kuikodolea nyumba ya kaka yake macho.Hakuamini kama Deo huyu aliyekuwa amefirisika na kuhamia kwenye ukulima wa mahindi leo hii anamiliki nyumba kubwa namna hiyo,hapohapo akapata funzo ya kuwa hakuna kitu kinachoshindikana chini ya jua!
“Hongera sana kaka Deo”
“Namimi pia,nina kushukuru sana.Kwa kunipa moyo”
“Bado siamini,Kaka Deo hii nyumba ni yako?Ama naota”
“Amini nakwambia”
Kilichokuwa mbele yao,ulikuwa ni ukweli mtupu!Mama Deo alivyoingia ndani na kumuona Marietha,akamsalimia kwa furaha lakini ilikuwa kinyume kwa Marietha kwani alikuwa akilia machozi,akapiga magoti mpaka chini.
“Naomba unisamehee Mama”
“Simama Mwanangu”
Marietha alihisi kumkosea kila ndugu yake Deo aliyemuona,ndiyo maana alienda mpaka chini kwa magoti.Mama akamuinua na kumkumbatia kwa nguvu huku akimpigapiga mgongoni asilie,siku hiyo Marietha alilia kama mtoto mdogo,alichofanya Mama ni kumuita Deo pia,wote akawa kumbatia kama kuku anavyofanya kwa vifaranga vyake!
Deo akashindwa kuzuia machozi yake,nayeye akaanza kulia ingawa hakuelewa analia kwa uchungu ama furaha.Historia ya maisha yake,alivyoikumbuka ilimgusa na kudhani wenda yupo ndotoni!Eveline nayeye akasogea na kujumuika nao.

******
Maandalizi ya sherehe yalipelekwa mkukumkuku,katika kamati ya maandalizi kuanzia mapambo na bajeti nzima ilisimamiwa na Mtui.Akamtafuta mpambaji maarufu na mkali kutoka Nchini Kenya Jijini Mombasa aliyeitwa Quin Thifa.Mtui, alitaka sherehe ya rafiki yake iwe nzuri yaani ibambe na watu wanywe na kufurahi mpaka wengine wabebe vyakula,hicho ndicho kilichotokea kwani alichangia kiasi cha shilingi milioni saba nzima,Deo akaweka yake!Marafiki wa Deo ambao zamani walimtenga kipindi alichokuwa amefulia, walivyosikia habari hizo walishangaa, hata hivyo Deo hakuwa na kinyongo nao,wakapewa kadi ya kuingia ndani ya sherehe hiyo, iliyoitwa ‘WELCOME BACK MY WIFE MARIETHA’Maandalizi yalianza,kamati ya chakula ikapiga hesabu,kamati ya vinywaji hawakuwa mbali.Kila kitu kikawa kwenye mstari.Siku mbili baadaye,Quin Thifa akawa ameingia nchini Tanzania kwa ajili ya kudizaini ukumbi ambao ulipangwa ufanyike hapohapo ndani ya jumba la Deo.
“Kuna jamaa yangu mmoja anaitwa Deo.Bado siamini macho yangu kama sasa hivi ametusua kwa mara nyingine!Nimejifunza kitu”
Deo akabadilika,akawa kioo katika jamii inayomzunguka.
Hiyo ilifanya vijana wanaokaa mitaani wafanye kazi kwa bidii, kwao ikawa kama chachu,kuna vijana walimfuata na kumuuliza siri ya mafanikio yake.
“Kufanya kazi kwa bidii na kupambana kila siku.Maisha ni vita,kamwe usikate tamaa.Na kitu kimoja,inabidi uwe na ndoto.Lazima ujuwe unataka kuwa mtu wa aina gani, hapo baadaye”
Huyu ni kijana ambaye alikuwa jirani yake,kipindi Deo anaishi Kimara miaka mingi sana!Mpaka leo hii Deo ana mvi kichwani,ndipo alipomtia machoni baada ya kuelekezwa ilipo nyumba yake kubwa mpya huko Upanga.
“Namimi ipo siku nitatusua”
“Jiamini,fanya kazi kwa bidii.Hakuna mafanikio ya bahati,ni juhudi zako mwenyewe”
Maswali kama hayo vijana wengi walimuuliza Deo,hakuwa na kinyongo aliwapa mbinu na kuwaaminisha kwamba kwenye kutafuta hakuna kitu uchawi,hivyo wasikate tamaa!
“Mimi mpaka nimezeeka sasa hivi,bado natafuta unaona mvi hizi.Sikukata tamaa.Unadhani ningeendelea kulalamika,ningefika wapi? Maisha ni kupigana maisha ni mapambano makali sana”
Mara Deo akageuka na kuwa mwalimu wa ujasiriamali,akafanikiwa kuwapandikiza vijana wa mtaani mbegu ya kushinda katika maisha yao,waliokata tamaa wakasimama tena.Deo akageuka na kuwa ‘role model’wa vijana wengi watafutaji.

******
Ilikuwa ni siku ya Jumamosi, tarehe 17 May.Siku hiyo Deo alikuwa amependeza,yupo ndani ya suti na mkewe Marietha, amevaa gauni zuri la kuwakawaka la rangi nyekundu,kwake siku hiyo ilikuwa ndio kama wanafunga ndoa sababu watu walikuwa wakimiminika kuingia ndani ya sherehe!Katika watu waliokuwa na furaha sana ni mwanamme huyu Mtui,muda wote meno yake yalikuwa nje!Katika sherehe hiyo hakuna mtu aliyekuwa amekaa chini yaani walikuwa wakitembea huku na kule na kupewa vinywaji,sherehe kama hizo wazungu huziita ‘cocktail’.Mziki mzuri ulikuwa ukipigwa wa Celine Dione ulioitwa ‘power of love’ hapo kila mtu alimshika mpenzi wake na kuanza kucheza naye taratibu.Deo na Marietha walikuwa wameshikana viuno,wanacheza mziki taratibu.
“Tumetoka mbali sana mke wangu.Nakupenda kuliko unavyodhani.Naomba usijutie kwa uliyonifanyia sababu kunifanyia vile,nisingepata hasira za kuinuka tena.Kwahiyo ninashukuru sana.Mungu akubariki”
Deo alizungumza taratibu huku akimtizama mkewe machoni,jinsi alivyokuwa bado mzuri.Japokuwa umri wa Marietha ulikuwa umeenda lakini uzuri wake ulikuwa palepale.
“Nakupenda mme wangu.Nakupenda sana,bila wewe mimi sio kitu kabisa.Sijui ningekuwa wapi sasa hivi bila wewe Deo wangu”
Sherehe ilizidi kupamba moto,na ilivyofika saa mbili usiku.Mshehereshaji maarufu aliyeitwa MC Swai, alikamata kipaza sauti na kumuomba Deo na Marietha watoke mbele na kuongea machache.
“Ahsante ndugu Mc.Ama kwa kirefu chake Msema chochote…”
Hapo watu wakacheka kidogo na kumuangalia Deo,aliyekuwa juu ya jukwaa dogo,kaulamba suti,kitambi kidogo kiasi, kimetokeza!
“Kwanza napenda kumshukuru Mungu kwa pumzi yake.Mimi nina amini siku zote pumzi ndio mtaji.Kitu kingine namuomba Mtui aje hapa mbele,huyu ni zaidi ya ndugu yangu.Katika shida zote nilizopitia yeye alikuwa bega kwa bega namimi mpaka leo hii ninavyoongea.Mama yangu mzazi pamoja na mdogo wangu Eveline,popote mlipo pia ningewaomba hapa!Siku zote nilikuwa nikiamini kwamba mafanikio ni bahati ya mtu….Nitaendelea baadaye kidogo lakini kwa sasa naomba nimpe kipaza sauti Mke wangu kipenzi Marietha!”
Deo alivyomaliza,akamsogezea kipaza sauti Marietha!Sio siri Marietha alivyotizama umati wa watu ulivyokuwa unamwangalia,alijisikia uchungu ajabu.Kumbukumbu nyingi zikawa zinamiminika kichwani kwake,akaona jinsi alivyokuwa binti mdogo!Kipindi walivyotoka mbali na Deo na changamoto kubwa walizopitia.
“Ahsante sijui niseme nini la..kini nina..kupenda sa…..”
Marietha hakuweza kumaliza hata robo ya maneno, aliyotaka kuongea,akaanza kumwaga machozi ya uchungu!Kila kilichotokea katika maisha yake,hakuamini kama ni kweli.Bado hakuwa tayari kukubali ya kwamba,Deo angeweza kumsamehee na wakarudiana, ndiyo maana alikuwa akilia machozi,hakuelewa kama ni machozi anayolia niya furaha ama niya misukosuko aliyopitia.



Siku zote kimfaacho mtu ni chake,Deo aliweza kumtibu Marietha na akarudiwa na akili zake,sasa ana akili timamu baada ya kuteseka na ugonjwa mbaya sana uliosababishwa na 'Stress' za maisha.Hakuna hata mmoja katika sherehe hiyo aliyeweza kuamini kwamba Deo na Marietha wamerudi tena kundini,mbali na hapo Deo amerudi tena kwenye chati.Walikuwa ni mfano wa kuigwa kwenye mambo mawili,safari ya maisha na uvumilivu katika Mapenzi.Katikati ya sherehe hiyo kulisikika minong’ono mbalimbali,wengi wao walikuwa wakimjadili Deo Karekezi na changamoto alizopitia.
“Jamaa alifungwa jela,unamuona yule Mwanamke aliyeingia ndani?”
Jamaa mmoja,aliyekuwa ndani ya sherehe hiyo, alimsemeza mwenzake.
“Yupi sasa?”
“Yule mke wake,aliyekuwa analia.Baada ya kupewa maiki”
“Ndio”
“Ndio huyo sasa mkewe.Mimi ningekuwa na mwanamke kama Yule,ningemuuwa.Jamaa alivyokuwa jela,mwanamke akamtema.Mbaya zaidi tetesi nilizosikia, alikuwa analiwa na mdosi mmoja, Tanga huko”
“Saa ikawaje?”
“Jamaa sijui ikawaje akatoka gerezani,kwenda kumfuata huyo mkewe.Akatolewa nje,unaambiwa jamaa alizimia siku nne mfululizo bila kuzinduka,akatundikwa dripu kumi..Ohoooo usifanye mchezo!”
“Weee!”
“Asikwambie mtu,balaa hilo.Usiombe yakukute,mapenzi ni mabaya sana”
Mazungumzo hayo yalizidi kupamba moto na hapohapo pia,chumvi iliongezwa na kachumbari ikajazwa.Wageni waalikwa waliendelea kupiga mvinyo,wakala na kushiba!Deo akaongea maneno machache ya kuwatia moyo, vijana waliokata tamaa,akawapandikiza mbegu ya ushindi,siku hiyo kila aliyekuwepo,alikuwa amepata kitu cha kujifunza.Marietha alikuwa ndani analia tu,Deo alivyoingia akawa ana kazi ya kumtuliza na kumwambia, kila kitu kipo sawa.
“De..o bado nau..mia”
“Unaumia nini mke wangu?Yamekwisha tayari”
Walikuwa tayari wapo Chumbani.Marietha yupo kitandani, ameinama analia kwa kwikwi.
“De..o sistahili kuwa na mwanamme kama wewe!Nimeshindwa, kusimama mbele za watu,naona aibu kwa matendo niliyokufan..nyia”
“Usijutie,kila kitu kilipangwa kiwe hivyo.Naomba utambue kitu kimoja,mimi ni mmeo.Ninakupenda,hata kama watu wakikuona vipi,tambua kuwa nipo nawewe bega kwa bega.Nakupenda sana Marietha”
Ni kweli,Maneno hayo yalitoka ndani ya mzizi wa moyo wa Deo,akasogea karibu zaidi akamuinua Marietha na kuanza kumfuta machozi, akitumia viganja vyake vya mikono,akamtizama kwa macho yalijoyaa husda,akaangalia midomo ya mkewe, ilivyokuwa ina rangi nyekundu na mizuri.Hapohapo, akili yake taratibu ikaanza kuhama na damu kuanza kumuenda mbio,hakujishauri kitu kingine chochote kile,akamvuta Marietha karibu na mdomo wake,akatoa ulimi nje na kuutumbukiza kinywani mwa Marietha,ambapo ulipokelewa vizuri, wakaanza kunyonyana ndimi.Deo,hakuwa mwenye wasiwasi tena kama hapo awali kwani walikuwa tayari wamepima afya zao na kila mtu alikuwa safi,hivyo walikuwa wana kila sababu ya kufurahia tendo analotaka kulifanya,kwani kwao lilihalalishwa.Akamsogeza taratibu Marietha kitandani,nayeye akaanza kupanda kwa juu yake.Akiwa hivyohivyo na viatu vyake,hakuna kitu kingine alichofikiria hapo zaidi ya kupitisha mkono wake nyuma ya gauni alilovaa Marietha,ambapo lilikuwa na zipu.Akaishusha,Marietha akaona isiwe tabu, nayeye akaonesha ushirikiano wa kutosha kwani aliinuka kidogo ili gauni alilovaa lipite vizuri,hata yeye alikuwa hajiwezi tena!Kitu kilichokuwa kinatokea,kilimpeleka mbali sana kihisia,ndiyo maana nayeye akaanza kumvua shati Deo kwa spidi.Akautoa mkanda,akamvua suruali.Kilichofanya suruali isitoke ni viatu, alivyokuwa amevaa Deo,akavitoa hapohapo.Ndani ya sekunde tano mbele, kila mtu akabaki kama alivyotoka tumboni mwa Mama yake,hapo waliendelea kushikana huku na kule,wakipashana.Hata hivyo Deo alikuwa ana kumbukumbu bado kwamba udhaifu wa Marietha upo kifuani,ndiyo maana alitoa ulimi wake na kuanza kulamba nido,hapo ndipo Marietha alipohisi raha zisizokuwa na mfano wake!Hakutaka tena mchezo huo uendelee,mwenyewe bila kuambiwa, akamchukua nyoka wa Deo na kumuweka kwenye ikulu,ambapo kilichofuata hapo wanandoa hawa walianza kufurahia,wakiwa katika ulimwengu mwingine wa huba!Saa nane za Usiku,ndipo walipomaliza mchezo huo,kila mtu akaonekana kuridhika kwa wakati huo.
“Nakuhaidi,sitokusaliti tena.Nimejifunza mengi sana Deo”
Marietha,alizungumza akiwa kifuani kwa Deo,anamkwaruza kwaruza na kucha zake.
“Tuyaache yaliyopita Mama”
“Nakupenda Mme wangu”
“Mimi pia.Kitu kingine,kesho tutaanza kumtafuta Abraham.Nishajua pa kuanzia tayari”
“Ulisema ulimuona?Ulimuona wapi?”
“Shule moja inaitwa Dokta Didas”
“Ulimjuaje?”
“Blood is thicker than water…Damu ni nzito kuliko maji,nilienda pale kusambaza chakula”
“Siku hizi una sambaza chakula?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Marietha,maskini ya Mungu! Bado, hakujua Deo anajishughulisha na nini.
“Ndio Marietha,nina mashamba ya Mahindi Bukoba huko,nitakupeleka siku ili ukaone.Pia, nina jenga Hostels kule Korogwe.Inabidi nikuoneshe kitu kimoja baada ya kingine ili unisaidie kusimamia mke wangu”
“Sawa Mme wangu”
Siku hiyo waliongea vitu vingi sana, hususani kuhusu maisha na namna ambavyo wangeanza kumsaka Abraham,siku itakayofuata.
Nusu saa, baadaye wakatoka nje huko walikuta wageni waalikwa wameanza kutawanyika tayari,hakukuwa na shida sababu waliambiwa wanywe walewe, mpaka kunakucha!

********
Harakati za kumtafuta Abraham mtoto wao kipenzi zilianza mara moja, baada ya kukucha na kupata kifungua kinywa,hapohapo Deo na Marietha hawakutaka kupoteza muda mwingine tena.Kila mtu alitaka kumuona Abraham,mtoto wao ambaye Marietha, aliamini kuwa alikufa miaka mingi sana iliyopita.Kila kitu kilichotokea, alijitupia lawama yeye mwenyewe na kujiita ni mwanamke mshenzi na mpumbavu kwani tamaa zake, ndizo zilifanya mpaka Abraham,atekwe na kutaka kuuwawa.Hata hivyo alikuwa akimshukuru Mungu kwa mambo yote yaliyotokea huko nyuma na kuamini kwamba kila kitu kinapangwa kwa sababu.Deo alianza safari mara moja, baada ya kulitoa gari nje,huku nyuma akimuacha Mama yake pamoja na Eveline nyumbani,wao wala hawakuwa na shida sababu walielewa kila kitu na Mama alimtia moyo kwamba watampata mjukuu wake.
“Deo usipompata itakuwaje?”
Marietha,akavunja ukimya wakiwa ndani ya gari.
“Tutampata tu,ninaamini hilo.Kwanini tusimpate?Nitatumia gharama yoyote ile”
“Walikwambia alisoma wapi?”
“O'levo,Makuburi secondary school baadae akahamishwa Dokta Didas”
Saa nne kasoro na dakika saba,Deo akawa amewasiri shule iliyosadikika kwamba alisoma Abraham, ndipo alipohamia Dokta Didas,matumaini yake yalikuwa ni kwamba, ajue pa kuanzia na aliamini huko wangempa muongozo!Alivyoweka gari,akafungua mlango akiwa na Marietha pembeni, mpaka ofisi za uongozi wa shule hiyo.
“Habari za hapa?”
Deo,akatoa salamu baada ya kumuona jamaa mmoja,ameshika madaftari mengi mkononi na fimbo,kivyovyote vile aliamini huyo alikuwa ni mwalimu!
“Nzuri tu mzee,shikamoo”
“Marahaba”
“Sijui nikusaidie nini mzee wangu?”
“Nahitaji kuzungumza na mkuu wa shule,sijui nimemkuta?”
“Ndio”
“Ofisi yake iko wapi?”
“Mlango wa tatu, hapo kulia”
“Ahsante”
Deo na Marietha wakafatisha maelekezo!Wakagonga mlango na kukaribishwa,nyuma ya meza walikumbana na Mzee mwenye mvi kichwani,mnene.Wakasalimiana kisha kukaa kwenye viti vya wageni.Deo,hakuwa na muda wa kupoteza, akaeleza shida yake!
“Anaitwa,Abraham Karekezi?”
Mwalimu akauliza huku akimtizama Deo!
“Yes”(Ndio)
“Alishafukuzwa hapa shuleni,ni muda kidogo”
“Sawa,hilo nalijua.Nachotaka kujua ni wapi anaishi?”
“Kuna mzee Mmoja anaitwa Chonga nilipoteza namba zake,na ndiye yeye aliyemuanzisha hapa.Lakini kwa msaada zaidi ngoja nikuitie mwalimu wake, aliyekuwa akimfundisha wenda atakuwa anafahamu”
Deo,hakudhani kama mambo yangekuwa mepesi namna hiyo,jambo alilokuwa akilitafakari na kitu alichokikuta vilikuwa ni viwili tofauti,kwani Mwalimu huyo mkuu hakuwa mwenye maswali mengi zaidi.Akasimama na kutoka nje,baada ya kurudi alikuwa na mwalimu mwingine wa kike,mdogo wa umbo!
“Hawa hapa,wanamtafuta Abraham.Yule mwanafunzi wako”
“Shikamoo…Shikaamoo”
Mwalimu akatoa salamu kwa Deo na Marietha.
“Marahaba”Wote wakaitikia kwa pamoja na kumtizama.
“Mr.Deo!Huyu anaitwa MWALIMU BEATRICE.Ndiye alikuwa mwalimu wake wa darasa”
Mwalimu Mkuu akatoa utambulisho mfupi.
“Beatrice,hawa wanamtafuta Abraham”
“Abraham Karekezi?”
“Ndio”
Moyo wa mwalimu Beatrice,ukapiga kwa nguvu mno!Jina hilo lilimkumbusha vitu vingi sana,hata yeye alitamani kukutana na mtu anayeitwa Abraham, siku zote lakini hakuelewa ataanzia vipi.
“Si alifukuzwa hapa”
“Ndio,wanataka kujua anapoishi”
“Sawa njooni ofisini kwangu”
Utaratibu ndio ulikuwa huo na sio kwamba Mwalimu Beatrice hakujua ni wapi Abraham,anaishi.Alifanya hivyo ili Mwalimu mkuu asihisi chochote.
“Abraham,anaishi Kawe Mwisho”
Kabla mwalimu Beatrice hajafika ofisini kwake,aliwageukia Deo na Marietha.
“Kawe?”
“Ndio”
“Unaweza kutupeleka?”
“Ah! Ah! Aaah!Ndio lakini nimesahau kidogo”
Kusema ukweli,hakuwahi kufika anapoishi Abraham lakini alijuwa anaishi eneo hilo linaloitwa Kawe,kivyovyote vile aliamini wangefika Kawe Mwisho,wangefanikiwa kumpata hata kwa staili ya kuuliza nyumba kwa nyumba!Kweli penye niya siku zote pana njia,saa saba kamili baada ya Mwalimu Beatrice kumaliza kazi zake,akaingia ndani ya gari na safari ya kwenda Kawe kuanza mara moja!Kitu alichofanya Marietha ni kuanza kumchimba mwalimu Beatrice.
“Kwahiyo alianza kusoma hapo form one?”
“Ndio Mama”
“Kwanini sasa alifukuzwa shule?”
“Ah ali ali ali ali si unajua ujana tena,watoto hawa wanakuwa”
Mwalimu Beatrice akataka kupindisha swali aliloulizwa,hakuwa tayari kuweka wazi na kusema kuwa Abraham, alikutwa anafanya ngono kwenye nyumba za walimu.
“Alifanya nini?”
Deo,akaingilia.Ilionekana nayeye alikuwa anasikiliza mazungumzo ya Mwalimu Beatrice na Marietha,jibu la Mwalimu Beatrice lilikuwa tata,halikueleweka vizuri ndiyo maana, akapunguza mpaka sauti ya redio ndani ya gari.
“Alikutwa kwenye nyumba za walimu”
“Ndio wakamfukuza?”
“Hapana”
“Sasa ikawaje?”
Deo akataka kujua zaidi.
“Alikutwa anafanya mapenzi na mwanafunzi mwenzake”
Deo akamgeukia Marietha na Marietha akamgeukia Deo,wakajikuta macho yao yamegongana na iliekea kila mtu kichwani kwake alisema ‘Mtoto wetu amekuwa’Kuanzia hapo, ukimya ukatawala.
“Ulisema ni Kawe mwisho?”
“Eeeee,ndio”
Mada ikawa tayari imebadilishwa na kilichofuata, hapo ni Deo kucheza na usukani mpaka walipofika Kawe Mwisho na kupaki gari kandokando kidogo.
Mitaa hiyo Beatrice aliamini kwamba Abraham ndipo anaishi,sababu kipindi walivyokuwa wapenzi alimueleza kwamba anaishi Kawe,ukishuka kituoni unaingia ndani ndani kidogo,hapohapo wazo kabambe likamjia.Akateremka ndani ya gari.Na kunyoosha mpaka kwenye genge,ambapo juu yake kulikuwa na samaki wa kukaanga!
“Mama shikamoo”
Mwalimu Beatrice,akasalimia.
“Marahaba,hujambo”
“Samaki, bei gani?”
Mwalimu Beatrice,akazunguka mbuyu kidogo.Niya yake haikuwa kujua bei ya samaki wala kununua,alitaka kidogo amzoee Mama huyo.
“Mia tano fungu,hawa elfu moja”
“Na hawa hapa?”
“Hao elfu mbili”
“Alafu nina shida nyingine?”
“Shida gani?”
“Namuulizia mzee Mmoja,anaitwa Chonga!”
“Chonga?Chonga yupi?”
“Mzee mmoja mfupi kiasi”
“Embu subiri”
Mama muuza Samaki,akamgeukia jirani aliyekuwa anapika samaki pia,akamuuliza!
“Mzee Chonga?Wewe humjui?Si Yule mzee mfanyabiashara wa Mahindi.Pale kwa Verynice”
“Kumbe ndio huyo?!”
“Ndioo”
“Anaishi wapi?Huyu binti ana shida naye”
“Pale kona kwenye ule mti wa Mkorosho,hapohapo”
Hapohapo Mwalimu Akawa amepata pa kuanzia,akamuaga Mama muuza samaki na kumuhaidi kwamba angenunua jioni yake,alivyofika ndani ya gari.Akamwabia Deo,kila kitu.
“Inabidi Marietha,uwende.Mimi ananifahamu,mara mwisho hatukuwa na maelewano mazuri”
Ilibidi Marietha,apangwe na amezeshwe maneno ya kuongea ili akazungumze na Mzee Chonga!Baada ya kila kitu kutimia akashuka ndani ya gari na kutizama,alipoambiwa aende!Baada ya kutembea hatua kama kumi hivi,akashtukia ameshikwa.
“Mariethaaa,Mambo vipi?Za masiku mke wangu”
Moyo wa Marietha ukapiga kwa nguvu, baada ya kugeuka nyuma na kuona sura iliyomkumbusha vitu vingi sana,hakuwa mwingine bali ni Michael Muganda.Mwanamme ambaye aliyewahi kuwa na mahusiano naye ya kimapenzi,miaka mingi iliyopita!




Ingawa umri wake ulikuwa umekwenda lakini ungemtizama ungedhani wenda ni mwanamke wa miaka 25-30.Marietha, alikuwa bado ana muonekano mzuri,shepu yake ilikuwa vilevile,amebinuka kwa nyuma.Uzuri wake ukawa palepale,hiyo ilitokana na matunzo ya Mmewe Deo Karekezi, ambaye alimtoa ndani ya shimo refu la matatizo makubwa,akamkarabati vizuri na kumfanya awe mrembo kwelikweli.Hiyo ndiyo ilimfanya mpaka Michael Muganda,apigwe na butwaa.Dera alilovaa Marietha lilikuwa limembana kiasi, ikafanya umbo lake lijichore,Michael akaanza, kumkagua kuanzia chini mpaka juu kwenye nywele.
“Unazidi kupendeza mke wangu”
Michael,akamwaga sifa nyingi.Huku akimmezea mate Marietha.
“Mimi sio mkeo”
Marietha,akajibu akiwa makini kabisa.
“Acha masihara basi,twende hapo mbele, tukapate japo soda.Sahau yaliyopita!”
“Michael,niache.Nina haraka”
“Nikuache vipi?Unaelekea wapi mpenzi wangu?”
“Mimi sio mpenzi wako”
Marietha,hakuwa tena na sababu ya kuendelea kusimama tena mahali hapo.Mbali na hapo, hakutaka kabisa kumpa nafasi Michael,hakupenda kurudia tena kosa,ndiyo maana akaanza safari ya kuelekea nyumbani kwa Mzee Chonga ili akakamilishe zoezi alilopewa la kumsaka Abraham,Michael akabaki akila kwa macho,akishuhudia namna ambavyo makalio ya Marietha yalivyokuwa yanatingishika kwa nyuma.
“Nitamsubiri hapahapa”
Michael,akasema na kwenda kukaa kwenye mgahawa mmoja uliokuwa pembeni.Niya yake ikiwa ni kumsubiri Marietha,alikumbuka mambo waliyofanya miaka mingi iliyopita, hivyo alitaka kupasha naye,jambo hilo aliamini litafanikiwa kwa asilimia zote mia moja,ndiyo maana akakaa na kuagiza Pepsi ya baridi ili apooze koo lake!
Marieta kama alivyoagizwa,ndivyo alivyofanya kwani alifika nyumba ya mzee chonga na kugonga,akagonga tena.Dakika mbili baadaye ndipo aliposikia kuna mtu ndani anatoka,akasuburi na kushusha pumzi nzito ya ndani kwa ndani!
“Karibu”
Mbele yake alisimama mwanamke mwenye umbo dogo kiasi,mweupe!
“Ahsante,samahani.Nimemkuta Mzee Mzee Mzee….”
Marietha akaonekana kama mtu anayevuta kumbukumbu ya jina lililomtoka!
“Mzeee.. mzeee.. Mzee Chonga”
“Hapana,ametoka lakini mimi ndiye mkewe.Unaweza kusema shida yako”
Verynice,mke wa Mzee Chonga!Akauliza kwa shari kidogo,ujio wa Marietha ulimfanya ajawe na wivu.
“Naweza kuingia ndani?”
“Ndio karibu,mimi ndiye mkewe”
Verynice,akajihami na wakati mmoja alijitapa.Baada ya hapo wakaingia ndani na kupita mpaka seblen,wote wakakaa juu ya makochi.Ukimya wa ajabu ukatokea,ilionekana kila mtu alikuwa akimtegea mwenzake aanze, kuongea!
“Kama nilivyokwambia,Mme wangu hayupo.Unaweza kusema shida yako tu”
Verynice,akavunja ukimya!
“Angekuwepo yeye,ingekuwa vizuri”
“Nimesema,hata mimi unaweza kuniambia.Kwani tatizo liko wapi?”
“Sawa”
“Enhee,nakusikiliza”
Verynice,akasogea karibu ili kusikiliza kitu anachotaka kusema mwanamke huyu aliyekuwa ni mgeni wa ghafla na isitoshe alikuwa akimuulizia mmewe,mbali na hapo alikuwa amependeza kupita kiasi!
“Mimi naitwa Marietha Deo Karekezi”
Moyo wa Verynice,ukapiga mkambo.Jina hilo, halikuwa ngeni kwake!Lakini hakutaka kuonesha mshtuko huo waziwazi!Marietha akaanza kujitambulisha,cha ajabu zaidi akaanza kuelezea tangu alivyofunga ndoa na mmewe Deo Karekezi, kanisani.Akazidi kuisogeza hadithi yake mbele zaidi,katikati ya maongezi yake akataja siku ambayo amejifungua mtoto anayeitwa, Abraham.
“Siku hiyo ilikuwa furaha sana.Kwa mara ya kwanza kujifungua Abraham baada ya kupata mateso,mme wangu alikuwa akinitesa na kuniita mimi mgumba, kisa nilikuwa sishiki mimba!Sio siri,jambo hilo lilinitesa sana….”
Sura ya Marietha ikaanza kubadilika taratibu, akaanza kuzungumza kwa huzuni huku machozi yakimlenga machoni mwake,mambo mengi yalikuwa yakipita ubongoni mwake na kukumbuka namna ambavyo alivyokuwa akiteswa na Deo Karekezi.Kilichomfanya aanze kumwaga machozi ni baada ya kumwambia kuwa alibakwa kipindi yupo nchini Ufaransa na Mwanamme katili, anayeitwa Amadour,hapo ndipo akashindwa kuendelea mbele zaidi,akainama na kuanza kulia sana.
“Mba..ya zaidi mme wa..ngu alilishuhud..ia tukio hi..lo baada ya kuachi..wa kutoka polisi..Akadh..ani nilifanya kusud..i nilium..ia sana,nilipojaribu kumuele..zea hakunielewa…”
Marietha,akaendelea huku akiongea kwa kwikwi,alizungumza kwa uchungu ajabu, ndiyo maana mashavu yake yalikuwa yakilowana na machozi.
Hata yeye hakuelewa ni kwanini anasema hayo kwani siku zote, ilikuwa ni aibu kubwa kwa mwanamke kusema amebakwa lakini kwa Mwanamke huyu ilikuwa ni tofauti kabisa,mambo aliyokuwa anayasema siku hiyo, Verynice alidhani anaangalia sinema ya kihindi,ndiyo maana hata yeye alianza kuona watu wawiliwawili, hiyo ni kutokana na machozi kuanza kujaa machoni,alimsikitikia mwanamke mwenzake.Alipoumia zaidi alivyosikia ya kwamba Mmewe alitaka kumtupa mtoto wa kizungu siku moja,hakuishia hapo moyo ulichoma, namna ambavyo Marietha alikuwa akiingiliwa kimwili na wanaume,waliojifanya kutaka kumpa msaada.Verynice akashindwa kuvumilia,akavuta kamasi na chozi likamdondoka hapohapo.
Nusu saa nzima Marietha, alikuwa akisimulia mkasa mzima,alivyomaliza tu.Akainama na kuanza kulia upya,akimshukuru Verynice kwa kumlea mtoto wake ambaye, aliamini kwamba kivyovyote vile, alikuwa anaishi hapo!
“Pole Marietha”
Verynice,akasimama hapohapo na kumsogelea Marietha,akamkumbatia na kumwambia kwamba mwanaye yupo salama na wanavyozungumza kwa wakati huo, yupo jijini Mwanza.
“Anapelekwa shule nyingine mpya”
Verynice,akaropoka.Hakuwa na sababu tena ya kukaa na siri hiyo, moyoni.
“Ninampenda kama mwanangu,nimemzoea sana”
“Ahs..ante,hakitoharibika kitu chochote kile,ataendelea kuwa mwanao tu”
Hakukuwa na haja nyingine ya kuendelea kusubiri,hapohapo Marietha akampigia simu Deo.Akafika ndani ya nyumba ya Mzee Chonga.
“Huyu ndio Mme wangu”
Jicho alilokatwa Deo liliogopesha,Verynice alimuangalia Deo Karekezi kwa macho makali yaliyojaa chuki,historia ya Marietha ilipanda mbegu ya kumchukia, hiyo ilimfanya Deo,ageukie upande wa pili.
“Huyu ndiye Baba Abraham”
Marietha,akasema tena.Niya yake ikiwa Verynice atoe salamu, lakini akala buyu!
“Ndiye alinifanya mpaka leo nimepona, nazungumza nawewe pia”
“Sawa,nashukuru kumfahamu”
Verynice akajibu kifupi,Deo akatoa mkono ili wasalimiane lakini mwanamke huyu Verynice, hakutoa mkono wake!Alichofanya ni kutoa simu na kumtafuta Mzee Chonga hewani ili afike nyumbani hapo.
“Kuna wageni,njoo”
Akakata simu,dakika kumi baadaye!Mzee Chonga,akafika.Kitendo cha kumuona Deo, Moyo wake ukapiga kwa nguvu.Zoezi la kumtuliza ili alainikie akalivaa Verynice,japokuwa kwa mara ya kwanza, haikuwa rahisi kama walivyodhani.
“Mpaka wapimwe DNA ya Abraham, pamoja na wazazi wake,hatuwezi kufanya vitu kienyeji enyeji”
Mzee Chonga,akahitimisha.
“Lakini,ni mtoto wao.Haina sababu ya ….”
“Yupo sahihi,hata mimi ningekuwa yeye.Ningefanya hivyohivyo!Hilo halina shida”
Verynice, alivyojaribu kutia neno,Deo karekezi akaingilia.Swala la Abraham kusafirishwa tena kutokea jijini Mwanza mpaka Dar es salaam ili kupimwa vinasaba, likawa limehafikiwa,taratibu za usafiri zilikuwa, juu ya Deo Karekezi.
“Nitamlipia tiketi ya ndege apande,hata kesho nipo tayari”
“Sawa”
********

Mawazo ya Karishma, yalikuwa kwa Abraham muda wote,tangu azaliwe hakuwahi kukumbana na hali ya utofauti kama hiyo!Kuna kitu kisichokuwa cha kawaida alikihisi ndani ya moyo wake,hiyo ilifanya kila wakati atake kumuona Abraham, jambo ambalo halikuwahi kutokea kabla.Cha ajabu na kilichomshtua zaidi ni usiku baada ya kulala,akamuota Abraham!Ndoto hiyo ilimuogopesha asubuhi kwani alivyozinduka asubuhi kulivyopambazuka,nguo yake ya kulalia ilikuwa imelowana kwa maana nyingine alikuwa ameota ya kwamba wanafanya tendo la kuzini na Abraham.Alivyotuliza akili yake,akakumbuka jinsi alivyokuwa na Abraham kitandani,anamtomasa!Hiyo ndiyo ikamfanya, azidi kupagawa zaidi na zaidi,hapohapo akakurupuka kutoka kitandani na kuchukua simu yake ya mkononi ili amsake Abraham,hewani!
“Kriii kriii”
“Krii kriii”
Simu ya Abraham,ilikuwa ikiita mfululizo bila ya kupokelewa.Mapigo ya moyo ya Karishma yalikuwa yakienda mbio,hakuelewa angemwambia nini Abraham endapo angepokea simu hiyo!Jambo hilo, lilifanya wakati huohuo atake kukata simu ili ajipange vizuri.
“Hallooo”
Upande wa pili ukasikika,sauti hiyo aliitambua sana.Ilikuwa ya Abraham,kijana aliyetokea kuusumbua mtima wake ghafla.
“Na na na..Naongea na Abraham?”
Karishma akapata na kigugumizi cha ghafla,sio kwamba hakujua anazungumza na nani.Lakini alijishangaa kuropoka!
“Ndio,nani mwenzangu?”
“Mimi Karishma”
“Karishma yupi?”
“Jana,ulipasua simu yangu.Hapa Midland hotel uk…”
“Okay,okay okay..Nimekukumbuka,mambo vipi?”
“Poa tu,uko wapi?”
“Naelekea airport”
“Airpot,unaenda wapi?”
“Dar es salaam”
“Kuna nini?Huendi shule tena?Una tabia mbaya.Hata kuniaga?”
“Family Matter, tu”
“Aya safari njema,tabia mbaya lakini.Mbona hukuniaga?”
“Sikuwa na namba zako”
“Safari njema,ukifika Dar,niambie”
“Sawa”
Karishma alivyokata simu,akashusha pumzi nzito ya ndani kwa ndani!Sauti ya Abraham, ilizidi kumpagawisha zaidi,akawa hajiwezi tena!
“Nahisi nimempenda Abraham..Mbona namuwaza namna hii?Ndio mapenzi yalivyo..Hapana,sitaki kumuwaza”
Karishma, alianza kubishana na moyo wake!Uliokuwa unataka muda wote,awe na Abraham!

**** *****
Uwanja wa ndege wa kimataifa jijini Dar es salaam,ulioitwa Mwalimu Nyerere,siku hiyo kulikuwa na watu wengi mno wakisubiri wageni kutoka nchi tofautitofauti.Miongoni mwa watu waliokuwa uwanjani hapo,walikuwa wakina Marietha,Deo,Mzee Chonga,Mwalimu Beatrice pamoja na Verynice.Wote walikuwa wakimsubiri Abraham kwa hali na mali.Kila mtu alitaka kumtia machoni,katika watu waliokuwa wanatamani Abraham afike mapema ni mwalimu Beatrice, ndiyo maana macho yake yalikuwa mlangoni,hakuelewa angefanya nini,endapo akimuona Abraham ametokeza.Kwa kitendo, alichokuwa anataka kukifanya,aliamini kabisa watu wangemshangaa lakini yeye hakujali kabisa, ilikuwa ni lazima ajitoe fahamu kwani bado alimuhitaji Abraham ndani ya moyo wake,ndiyo maana muda wote alikuwa bega kwa bega na Familia ya Abraham ili ahakikishe wanakwenda sambamba!Moyo wa Marietha pia ulikita kwa nguvu sana,jambo la Abraham kuwa hai, kwake alilifananisha na muujiza mkubwa sana!Ndiyo maana, moyo wake ukawa una shauku kubwa ya kumtia mwanaye machoni,wakati mwingine, alitamani kuingia ndani ili kumtoa nje kwani mpaka dakika hiyo ndege iliyokuwa inatoka Mwanza ilikuwa tayari imetua,ilielekea abiria walikuwa katika ukaguzi fulani fulani,uliowafanya wachelewe kutokeza.
“Abrahaaaaaaaam!”
Ukelele huo,aliuachia mwalimu Beatrice kwa furaha bila kujali.Hiyo, ilifanya watu wote wamuangalie!Hakujali kwani ndiye alikuwa wa Kwanza kumuona akiwa langoni anaburuza begi ametokeza.Moyo wake ulikuwa ukipiga kwa nguvu,akawapangua watu waliokuwa mbele yake na kuzunguka upande wa pili,bila kujifikiria kitu chochote,akamsogelea na kumrukia,almanusura amdondoshe!
“Nimefurahi kukuona mpenzi.Nimekumisi”
Mwalimu Beatrice,alizungumza maneno hayo kwa furaha!Hiyo ilimfanya Mama Maria aliyekuwa pembeni ya Abraham,apigwe na butwaa!Wivu ukamjaa,akamkata jicho kali Mwanamke huyu,aliyemng’ang’ania Abraham,barafu wa moyo wake!




Hali ya sintofahamu inamkumba Mama Maria,akiwa nyuma ya Abraham ameshika mkoba wake, anamtizama Mwalimu Beatrice ambaye kwa takribani sekunde tisa, alikuwa amemnng’ang’ania Abraham,wivu ulimjaa lakini upande mwingine wa nafsi yake, unamwambia ya kwamba wenda mwanamke huyo atakuwa ni ndugu yake kwani alivyopiga jicho pembeni, alimuona mzee Chonga akiwa na Verynice.Hata hivyo tangu wanaanza safari, kutokea jijiji Mwanza Abraham alimueleza kuwa, alipigiwa simu na Mzee Chonga akimtaka arejee Dar es salaam kwani kuna jambo la muhimu na dharura,hapo ndipo walipoanza safari wakipanga kuwa wakifika Mwalimu Nyerere, wawazuge na kuwaambia ya kwamba walikutana tu ndani ya ndege.
“Abraham pole na safari mwanangu”
Verynice,Mwanamke mwenye roho safi aliyemlea Abraham tangu akiwa mtoto alimsogelea karibu na kumpokea begi huku akiwa mwenye tabasamu pana,Marietha bado alikuwa kama mtu aliyepigwa sindano ya ganzi,anamshangaa Abraham, hakutaka kuamini ndiye mwanaye kwani alikuwa mkaka mkubwa kabisa,alivyotaka kuongea akahisi kama mdomo wake umejaa mate.Kwa Abraham,alikuwa kama amepigwa na bumbuazi la waziwazi, baada ya kuangaliana na Marietha,sura ya mwanamke huyo ilifanya ubongo wake urudi nyuma kwa kasi ya kompyuta isiyokuwa na mafaili.Akakumbuka namna alivyokuwa mdogo wakiwa na William,hakuwa ana uhakika kama anayemuona ni Mama yake ama amemfananisha,japokuwa aliachwa akiwa yu mdogo lakini memori ya kichwa chake ilikuwa imehifadhi picha ya mwanamke huyo.
“Maaa..maaaaa”
Abraham,akaita huku akimtizama Marietha.Kila mtu akabaki kimya akimtizama kwani Abraham alisogea karibu kabisa na Marietha.
“Abraham”
Marietha nayeye akaita,hakuweza tena kujizuia, hapohapo akapata nguvu za ajabu, akatembea kwa kasi na kumfikia Abraham,akamkumbatia kwa nguvu huku akimwaga machozi.Mwanaye alimkumbusha vitu vingi sana, alimkumbusha maisha ya msoto aliyopitia huko nyuma kipindi amefukuzwa na Deo!
Bado, hakutaka kuamini kama mtu aliyekuwa mikononi mwake ni Abraham,mwanaye kipenzi,wakati mwingine alidhani wenda ni mazingaombwe tu.
“Nisa..mehe mwanangu”
Marietha alikuwa ana kila sababu ya kuomba msamahaa kwa mwanaye kwani yeye ndiye alikuwa mkandarasi wa kila kitu kutokea, miaka ya nyuma. Akafanya mpaka Abraham na Wiliam watekwe nyara na Tycoon Maximo, kisa tamaa zake za pesa.Maisha yake ya nyuma yalikuwa yanatisha, mpaka mwenyewe akayaogopa.Isingekuwa Deo Karekezi kutokea na kuwaaambia waingie ndani ya gari wenda wangekesha,wote wakaanza safari ya kuelekea kwenye maegesho ya magari.
“Mama Maria!Nawewe ulikuwa Mwanza?”
Mzee Chonga akavunja ukimya,uwepo wa Mama Maria, ulifanya aibue swali.
“Nilikutana na Abraham ndani ya ndege”Alidanganya.
Kufuatia hapo,Mama Maria akatembea mpaka pembezoni, kulipokuwa na taxi nyingi,akaita moja wapo huku akiwaacha wakina Mzee Chonga wanaingia ndani ya gari la kifahari aina ya Volks Wagen,hata yeye mwenyewe alilitolea udenda, lilikuwa ni gari kali balaa.Furaha aliyokuwa nayo Deo,haikuweza kuelezeka kiwepesi,hatimaye alikuwa ameipata familia yake, baada ya kuitafuta kwa muda mrefu kidogo!
“Tunaelekea wapi sasa?”
Mzee Chonga,akaanza kuhoji baada ya kuona Deo anatoka nje ya lango la uwanja wa ndege.
“Kwangu”
Hakukuwa tena na maswali mengi zaidi,kuanzia hapo kilichokuwa kinasikika ni sauti ya mziki wa redio uliokuwa ndani ya gari.
Kutoka uwanja wa ndege uliokuwa Kipawa, mpaka anapoishi Deo Karekezi,Upanga. Iliwachukuwa dakika hamsini nzima,hiyo ni kutokana na Deo kulipitisha gari lake juu ya lami,alilipenda gari lake jipya, ndiyo maana hakutaka kupitia njia ya mkato yenye mawe na mabonde.Walivyofika mtaa wa kwanza,wakaingia wa pili, hapo akazungusha usukani na kusimama nje ya geti kubwa, lenye rangi ya kijivu kwa juu,chini nyeupe!
“Ngoja nikafungue geti”
Hawakuwa na mlinzi,ndio maana Marietha akateremka kutoka ndani ya gari,akazama ndani na kulifungua geti.Mzee Chonga,akabaki anatumbua macho,mbele yake alikumbana na jumba kubwa la kisasa na nje kulikuwa na uwazi mkubwa,ambapo pembeni yake kulikuwa na bustani ya maua iliyopambwa kwa ustadi bomba maalum, linarusha maji.Hapo ndipo alipogundua kuwa Deo Karekezi, hakuwa mwanamme wa mchezomchezo,gari likaingia mpaka ndani.Mzee Chonga, akazidi kupepesa macho yake huku na kule,alivyoshuka na kuangaza kwa nyuma akaona bwawa la kuogelea.Si yeye aliyestaajabishwa na jumba hilo, hata Mkewe Verynice pamoja na Mwalimu Beatrice wote waliduwaa!
“Karibuni jamani,jisikieni mpo nyumbani”Deo akasema huku akitabasamu!
Walivyofika seblen ndiyo wakapigwa na butwaa kabisa,seble ilikuwa kubwa mno.Ukutani kuna televisheni kubwa sana,makochi ya kuvutia na juu kuna picha kubwa ambayo,sura ya Deo akiwa na Marietha wakiwa kanisani wanafunga ndoa ilionekana!Kila mtu alimshangaa Deo kwenye picha na jinsi alivyo kwa wakati huo,vilikuwa ni vitu viwili tofauti.Kwa wakati huo alikuwa kidogo amezeeka ana mvi kichwani, pichani alikuwa kijana mdogo tu.
“Karibuni jamani.Mzee Chonga vipi?Vinywaji gani mnatumia?”
Deo akauliza,hakutaka wageni wake, wabaki vinywa vimekauka ilikuwa ni lazima, wapooze makoo yao!
“Mimi maji tu”
“Mzee mwenzangu.Maji ya nini tena?Una dozi?Hapa kuna kila kitu”
“Basi niletee kinywaji kinachonifaa mimi”
“Hapo umenena.Shemeji pale?”
“Mimi juisi”
“Beatrice”
“Juisi tu”Kila mtu akasema alichotaka kunywa,Abraham pia akataka juisi.
Marietha siku hiyo alikuwa ‘sharp’ sana, kila kitu alikisikia akiwa jikoni, ndiyo maana akaanza kutafuta trei kubwa ili aweke vinywaji.
“Mariethaa”
Deo,akamuibukia jikoni hukohuko.Ilionekana, alitaka kumwambia kuhusu vinywaji vya wageni.
“Abee”
“Ile wisky Vat 69.Iko wapi?”
“Baba Abraham,unataka kuwapa hiyo?!”
Marietha,akauliza kwa mshangao wa waziwazi huku akimtizama mumewe usoni.
“Ndio”
“Hapana bwana,hiyo kali.Sindo ile mpaka uwashe moto?”
“Hiyohiyo ndiyo”
“Hapana Darling,tafuta nyingine”
“Namaque labda”
“Itakuwepo kweli?”
“Nikuulize wewe,maana mara ya mwisho nilikuacha nayo, unaangalia movie”
“Ilibaki nusu”
“Iko wapi?”
“Chumbani”
Deo,akaingia chumbani.Na kilichofuata hapo,wote wakawa katika hekaheka za kuwaandalia wageni vinywaji.Kila kitu kilivyokamilika,wakawekewa mezani!Kila mtu akachukuwa chake.
“Mzee mwenzangu,hii itatufaa.Kwa sisi wazee!Inapunguza mafuta mwilini”
Deo,akamwambia Mzee Chonga kwa staili ya kumtania kidogo kwani alionesha tabasamu kidogo, hiyo ilimfanya Mzee Chonga ajisikie yupo nyumbani kwake.
“Mimina bwana,mkulima hachagui jembe”
Walivyomimina,wakatulia kidogo.
“Mariethaa”
Deo akaita,Marietha alikuwa jikoni ilibidi atokeze nayeye.
“Njoo tupige cheers mke wangu”
Alichotaka Deo,ndicho kilichotokea kwani wote walisimama wima, wakagonganisha glasi kwa pamoja na kusema ‘Cheeeeeeeers’ kisha kuanza kunywa.Kama ilivyokuwa tabia ya Deo kwamba ukiwa naye ni lazima ufurahi,akaanza kupiga stori za hapa na pale.
“Kuna siku nakumbuka zamani kidogoo”
Akaanza stori huku akikaa vizuri,kila mtu akamwangalia.
“Nilikuwa na rafiki yangu mmoja,anaitwa Bariki.Alikuwa ni mchaga,tulikuwa tunasoma darasa moja.Nakumbuka ilikuwa darasa la saba ama sita hivi,kitu kama hicho….”
Jinso Deo alivyokuwa anaongea,wageni wakaanza kutamani aendelee na stori kwani aliongea, akiwa amejiachia na kuonesha tabasamu nene.
“Huyo rafiki yangu Bariki,mlevii kweli.Tulikuwa tukitoka shule,tunaenda kulewa.Na Ndiye alinifundisha kunywa pombe!Siku hiyo tukaenda kufakamia pombe za jeshini…Hiyo siku sitoisahau…”
“Jeshini?Ilikuwaje tena?”
Mzee Chonga,akataka Deo aendelee na hadithi kwani alitaka kujua, mkasa uliomkuta kambini.
“Bariki,akalewa akaanza kutukana.Alivyokuwa mshenzi wa tabia.Akasimama juu ya meza.Akasema wanajeshi wote mna mavi……”
“Ha! Haa! Haa! Haaa! Haaaa! Haaaaaaaa!”
“Ha! Haa! Haaa! Haaa! Haaaa!”
Baada ya hapo kila mtu akaangua kicheko,Marietha akacheka mpaka machozi yakaanza kumtoka kwani tangu amjue Deo, hakuwahi kuambiwa stori ya namna hiyo kwake ikawa kama kibonzo!
“Subiri sasa nimalizie,Mwanajeshi mmoja wa pembeni.Akasimama.Akamuuliza,wewe mtoto unasema nini?Unajua alichojibu Bariki....”
“Alimjibu nini?”
“Hasa hasa wewe,ndiyo una mavi mengi tumboni…Kilichofuata hapo,Mungu ndio anajua!Ndiyo maana mpaka leo,wanajeshi sina hamu nao tena”
“Ha! Haa! Haa! Haaaa!Waliwafanya nini?”
“Aisee,wale jamaa msicheze nao”
Dakika kumi baadaye, Mama Deo pamoja na Eveline wakawa wameingia,ugeni ukawa umeongezeka wakasalimiana kwa furaha.Kitendo cha Mama Deo kumuona Abraham,akajuwa moja kwa moja ni mtoto wa Deo,kwani damu yake aliijua vizuri sana!
“Mama karibuni sana”
“Ahsante mwanangu,naona umekuja na Baraka”
“Kwanini Mama?”
“Wageni ni Baraka mwanangu”
Mama Deo nayeye,akaingilia kati wakaanza kupiga soga.Marietha hakucheza mbali na jiko,sababu hakutaka wageni waondoke hivihivi, ndiyo maana alianza kukarangiza akiwa mwenye furaha kupita kiasi siku hiyo.
Hakuelewa ni kwanini ana furaha kupindukia, lakini alielewa ni kwasababu ya kurudiana na Deo, sambamba na kuwa na mtoto wake Abraham pia,kwa heshima ya wageni ilibidi atoe nyama ya kuku iliyokuwa ndani ya friji,akaanza kucheza nayo jikoni,chakula kilivyokuwa kinaendelea kuiva huku Seblen wageni walizdi kupamba moto kwa kucheka na kufurahi.
“Abraham,ni mtoto mmoja msikivu sana!Nadhani upole wake,ameridhi kwa Mama”
Mzee Chonga,akaanza kumzungumzia Abraham, baada ya kuifikia glasi ya tatu ya pombe, ambapo akili yake ilionekana kuchangamka.
“Kwanini?”
“Mama yake,sio mwongeaji”
Hapo alimaanisha Marietha.Maongezi yaliendelea na baada ya hapo Deo aliifata Album ya picha,akawa anamuonesha Mzee Chonga, picha za Abraham akiwa mdogo kabisa.
Hiyo ilifanya Mzee Chonga, asiweke tena kipingamizi,hakuwa ana haja tena ya kuipima familia hiyo DNA.Picha alizoona zikawa jibu tosha kabisa,ilivyofika mchana, wakatengewa chakula mezani waakanza kula.
Kila mtu alikisifia chakula hicho namna ambavyo kilivyokuwa kitamu,ilivyofika saa kumi jioni ilibidi Mzee Chonga,Verynice,Deo pamoja na Marietha watoke nje kidogo,ilielekea kuna jambo walitaka kuteta.Hakuna kitu kingine walichozungumza zaidi ya kufanya makabidhiano na Abraham.Shukrani, alizotoa Deo kwa Mzee Chonga,hazikuweza kuelezeka kiwepesi.
“Abraham,ataendelea kuwa mtoto wenu tu.Nitamwambia awe anakuja kuwasalimia,tafadhali msiogope kututembelea hapa!Nasisi tutakuwa tunakuja”
Deo akatoa neno.Kilichotokea hapo ni kupeana mikono na kukumbatiana,akaitwa Abraham na kuelezwa kila kitu kilivyokwenda,alionekana kufurahi lakini upande mwingine alinung’unika kwani aliizoea sana familia ya mzee Chonga,kwake ilikuwa ngumu kutenganishwa nayo ingawa alikubali matokeo, hakukuwa na namna ya kuzuia kilichopangwa,hatimaye Abraham akawa amerudi mikononi mwa Wazazi wake,rasmi!

*******
Wahenga waliosema ‘Penzi ni kikohozi,kulificha huliwezi!’Walikuwa sahihi kabisa na sio siri,msemo huo haukuwahi kumuacha mtu yoyote yule salama.Karishma alikuwa katika gereza la mapenzi,hajiwezi amegeuka na kuwa mfuasi,akawa teja kabisa.Hali aliyokuwa nayo ilimuogopesha mwenyewe!Vitabu vya hadithi za mapenzi mbalimbali vya akina Eric Shigongo,Tatu Kiondo,Frank Mansai,Zuberi Mavugo,Hussein Molito.Ambazo alisoma watu, wakijiua ama kurukwa na akili kisa mapenzi, ilimfanya akubaliane na hali,hapo nyuma aliwashangaa watu hao na kuchukulia kwamba ni vitabu tu vya kubuni,leo hii ilikuwa kwake.Hakuelewa ni namna gani imetokea lakini alihisi kumpenda sana ABRAHAM KAREKEZI.
Hilo lilikuwa ni pembe la Ng’ombe,halikufichika kabisa, sababu mpaka wanatoka Jijini Mwanza kurudi Dar es Salaama na Mama yake,hakuweza kula.Mawazo yake yalikuwa kwa Abraham mbaya zaidi,alivyokuwa akipiga simu,hazikupokelewa hata kidogo!
“Karishma una nini?”
Siku hiyo Mama aliingilia kati,ilibidi ahoji.Karishma alionekana kuwa mwenye mawazo mengi mno,hata chakula hakumaliza siku hiyo,akaenda chumbani kwake na kujitupa.
“Nipo sawa Mama”
“Una uhakika?”
“Ndio Mama”Mama,akatoka!
Hapohapo akachukuwa simu yake na kuingia ‘WatsApp’ kumtafuta Abraham kwa mara nyingine kwani meseji zote alizotuma,hazikujibiwa.Kilichomuumiza zaidi mtima,zilikuwa zinaonesha alama za tiki mbili za rangi ya bluu,kumaanisha kwamba meseji zote alizomtumia Abraham ameziona,hilo ndilo lilimuuma zaidi na zaidi.
“Simtafuti tena,hii ndio meseji ya mwisho.I can’t do this anymore.This is bullshit ”
Karishma alijisemesha na kuanza kuandika ujumbe mwingine.
“Hii,Abraham.Mimi nalala nyt nyt.Imiss you”
Karishma akatuma ujumbe na kutafuta emoji ya kopa,akaiweka mwishoni pia.
Kilichomshtua zaidi ni baada ya kuona tiki mbili na Abraham, alikuwa ‘online’Akasikilizia kwa sekunde tano nzima lakini meseji yake,haikujibiwa,moyo ukamuuma ajabu.Akasusa na kutupa simu pembeni,akajikita kwenye mawazo,akiapia ya kwamba hatomtumia tena meseji Abraham,mara ghafla simu yake ikaanza kuita,moyo wake ukapiga paa!Alivyoangalia juu ya kioo,akakasirika baada ya kuona jina ‘Razack’alimtambua sana,mwanamme anayemsumbua akimtaka kimapenzi,hapohapo akakata simu.Lakini ikaita tena,akaikata,mara ya tatu ilivyoita,akaipokea kwa haraka na kuiweka sikioni,tena kwa hasira.
“Razack,nimekwambia unikome.Usinipigie tena simu.Iwe mwanzo na mwisho,don’t call me don’t text me again ume…”
“Karishma,mimi Abraham”
Kusikia hivyo,Karishma akatoa simu kwa haraka na kuangalia juu ya kioo,moyo wake ukapiga mkambo, baada ya kuona jina la Abraham juu ya kioo chake cha simu!


“Samahani,Abraham.I'm so sorry,sikujua kama ni wewe!Kuna mkaka ananisumbua sana”
Karishma alianza kujieleza, akijaribu kujitetea.
“Poa,usijali.Hujalala tu?”
“Ndio,nilikuwa nasubiri meseji yako.Tangu jana hujibu meseji zangu”
“Nilikuwa bize,home.Alafu jana simu niliacha nyumbani,ndiyo maana ukaona kimya namna ile.Uko poa?”
“Mimi niko poa,nakumisi sana.Unaishi wapi?Japo nije kukuona”
“Upanga”
“Upanga sehemu gani?”
“Shule ya Azania ukishuka,kuna mtaa wa kwanza pale una lami.Mitaa siijui vizuri lakini ukifika Azania mimi nitakuja kukufata”
“Nije lini?”
“Nitakwambia”
Jinsi Abraham alivyokuwa akimjibu simuni,ilimfanya ajisikie faraja sana.Ilikuwa, wazi kabisa kama angekuwa ana uwezo wa kuingia ndani ya simu na kumfuata Abraham alipo angefanya hivyo,lakini muujiza huo usingewezekana kamwe.
“Abraham”
“Yes”
“Sasa hivi unafanya nini?”
“Nipo tu kitandani,nacheki movie”
“Movie gani?”
“Avatar”
“Movie hiyo ni nzuri sana,nije tuangalie wote?”
“Usijali”
“Abraham,una sauti nzuri”
“Ahsante”
“Wifi anafaidi”
Karishma akaanzia mbali kidogo,taratibu alianza kumchimba Abraham.Aliamini kwa neno hilo angepata jibu la kwamba kama Abraham ana mahusiano ya kimapenzi ama yupo ‘single’mapigo yake yalianza kwenda mbio kwani siku hiyohiyo alitaka kumwambia Abraham kitu kinachomsumbua ndani ya mtima wake,ilikuwa ni lazima amuelezee namna ambavyo anateseka kila kukicha.
“Kawaida tu”
Abraham,akajibu lakini jibu hilo halikujitosheleza.Karishma akabaki njia panda,jibu la Abraham lilikuwa tata.
“Kawaida waaapi?Be honest,wifi anafaidi si useme tu”
Karishma akazidi kutingisha kiberiti.
“Sasa mimi nitajuaje?”
“Yupo lakini?”
“Yes yupo”
“Sipati picha alivyokuwa mzuri”
“Yes,yah”
“Nitumie picha zake nimuone”
“Karishma,usiku mwema.Wacha nilale,tutaongea kesho nimechoka sana”
Abraham akasema,na ni kweli namna alivyokuwa anazungumza simuni ni wazi kabisa sauti yake ilisikika kwa kukwaruza kwa mbali,Karishma akawa muelewa akaaga kishingo upande huku moyo ukimuuma ajabu,aliendelea kutamani kuisikia sauti ya Abraham, wakati wote simu ilivyokatwa ilimuacha Karishma akiwa katika dimbwi la mawazo mengi mno,kichwa chake hakikujaa mtu mwingine isipokuwa Abraham tu,wakati mwingine alitamani angekuwa naye pembeni ya kitanda chake!Kuanzia siku hiyo Karishma na Abraham walikuwa wakiongea kila siku usiku mpaka mazoea yakajenga tabia.
Kitu kilichokuwa kinamuuma Karishma ni kimoja,kila ikifika saa mbili simu ya Abraham inakuwa bize mpaka saa nne za usiku,siku hiyo akajitosa kimasomaso na kutaka kujua Abraham anazungumzaga na nani ikifika mida hiyo.
“Ni nani unaongeaga naye usiku Abraham?”
Karishma alimuuliza Abraham simuni,tena kwa ukali kidogo.Hakutofautishwa na mwanamke anayemuuliza mmewe kwani aliuliza kwa kujiamini mno,hiyo ilimfanya Abraham atulie kidogo!
“Abraham,talk to me”
“Na girlfriend wangu,nilikuwa naongea na mpenzi wangu.Ni vibaya kwani?Alafu unaniuliza hilo swali, kama nani labda?”
Moyo wa Karishma uliuma ajabu,akahisi kama amechomwa sindano ya ganzi,akaganda!Machozi yakaanza kumlenga,akasitisha kuzungumza na Abraham.
“Halloo,mbona kimya?”
“Abraham,usiku mwema…tititi”
Hapohapo Karishma akakata simu,alivyokiweka kichwa chake juu ya mto akaanza kulia machozi,kitendo cha Abraham kumfokea ukichanganya na majibu yake yaliyomfanya ajisikie wivu ilipelekea mpaka kichwa kimuume,sio siri ilikuwa ni wazi kabisa Karishma alikufa na kuoza juu ya Abraham, lakini bado hakuelewa ni namna gani amwambie,aliogopa kutongoza na hakujua namna wanavyofanya,alimshangaa Abraham anavyomjibu majibu ya mkato wakati ndani ya simu yake kulikuwa na meseji zisizopungua mia mbili za wanaume tofauti tofauti,wakimtongoza.
“Abraham nakupenda,mbona unanitesa namna hiii?”
Karishma alizungumza mwenyewe,kichwa chake kilikuwa kinawaka moto, kutokana na mawazo mengi aliyokuwa nayo juu ya kijana huyo,mzuri wa sura aliyetokea kuunyanyasa mtima wake ghafla sana.Usiku mzima hakupata hata lepe la usingizi,alikuwa akimuwaza Abraham tu.
“No,nitabaki hivi mpaka lini?Hata akinifikiria vibaya ni sawa tu”
Karishma akajisemea mwenyewe usiku,ukweli ni kwamba alivyokata simu hesabu zake zilikuwa wenda Abraham atapiga na kuuliza kulikoni kwanini umekata simu?Lakini matokeo yake hakuna simu wala ujumbe wowote ule ulioingia, hapo ndipo akazidi kuumia zaidi,moyo wake ukamsukuma achukuwe simu apige kwani alijisikia kuzungumza na Abraham kwa mara nyingine ingawa usiku ulikuwa mwingi.Hapohapo, akaikwapua simu yake na kuruka hewani.
“Mtumiaji wa simu unayempigia,anaongea na simu nyingine h…..”
Hapo ndipo Karishma akahisi kama kuna mtu kaingia ndani ya moyo wake,anaukamua!Laini ya simu ya Abraham ilikuwa inatumika kwa maana kwamba ilikuwa ni lazima alikuwa kwenye mazungumzo na mtu mwingine,jibu lililomjia harakaharaka ni lazima atakuwa anazungumza na mwanamke wake,jambo hilo lilimfanya ahisi kuchanganyikiwa zaidi.Japokuwa alijuwa inatumika,akapiga tena na tena,aliendelea kufanya zoezi hilo mpaka dakika kumi zikapita,ndipo Abraham akapokea simu.
“Abraham…..”
Karishma akaita kwa sauti ya unyonge.
“Yes”
“Mbona unanitesa sana?Naumia”
“Kwanini?”
“Sijui lakini naumia sana,nikisikia simu yako inatumika”
Kuanzia hapo ukimya wa kama sekunde tatu ukatokea!
“Hallo Abraham,mbona huongei?”
“Nakusikiliza”
“Nakwambia naumia,najua wewe ni mzuri.Kila siku unatongozwa nipe japo namimi muda wa kuzungumza nawewe”
“Karishma”
“Abee”
“Tatizo nini?”
“Naomba usinifikirie vibaya lakini”
“Nambie tu,sitokufikiria vibaya”
“Sijawahi kuwa katika hali hii,tangu nizaliwe”
“Hali gani?”
“Nakupenda Abraham,naomba uwe mpenzi wangu”
Karishma alizungumza kwa hisia,mpaka akafunga macho yake, haikujulikana aliona aibu ama ndiyo mahaba niue!
“Niwe mpenzi wako?!Mimi?Hapana siwezi”
Abraham akaongea,maneno hayo yakageuka na kuwa mishale ya moto,ikamchoma Karishma moyoni.Akajihisi kama yupo uchi wa mnyama tena mbele za watu,kitendo cha Abraham kumchomolea kilimfanya ahisi kizunguzungu cha ghafla.
“Abraham please,nipo tayari kufanya chochote kwa ajili yako”
“Hapana siwezi,kama huna kitu kingine cha kuzungumza.Kata simu”
“Abraham…”
“Au,nikate simu mimi?”
“Hapana Abraham”
“Basi,usiku mwema”
Huo ndio ulikuwa msimamo wa Abraham,Karishma siku hiyo alilia kama mtoto mdogo.Mpaka kunakucha,hakuweza kusimama kutoka kitandani.Hata mama yake alivyoingia chumbani kwake kumuamsha,ikashindikana.
“Chai hunywi leo?”
Dokta Katrina,akauliza.
“Nitakunywa”
Karishma akajibu akiwa bado yupo kitandani,amejifunika na shuka.
“Unaumwa au?”
“Hapana Mama”
“Mbona macho yamevimba?”
Haukuwa utani,macho ya Karishma yalikuwa yamevimba na mekundu,hiyo ni kutokana na kumlilia Abraham usiku kucha.
“Kawaida tu Mom,sijalala jana nilikuwa naangalia movie”
“Usipende kuangalia movie mpaka asubuhi,sio kitu kizuri kwa afya yako”
“Sawa Mom”
“Aya baadaye,utamwambia Dada akupikie soseji.Jana nilinunua Pizza,zipo kwenye friji”
Karishma hakujibu chochote,vyakula hivyo alivipenda siku zote lakini siku hiyo hakutaka kabisa kusikia kitu kinachoitwa chakula,aliamini kabisa hakitopita.Mawazo yote yalikuwa kwa Abraham,aliwaza vitu chungu mzima.Kifupi moyo wake ulikuwa maututi na daktari alikuwa ni Abraham peke yake.

********
Kitu kutongozwa na Wanawake,ama wasichana wazuri kwa Abraham ilikuwa kawaida sana.Ndiyo maana alidiriki kumtolea nje msichana mmoja mrembo ambaye alikuwa katika mashindano ya miss Tanzania aliyeitwa Rehema Kiswabi,starehe ya ngono kwake halikuwa jambo alilolipa kipaumbele sana katika maisha yake,sababu aliamini alichokuwa nacho Mama Maria na wanawake wote wanavyo,hata hivyo alianza kuijua nguo ya ndani ya mwanamke akiwa bado mdogo sana,kifupi alitokea kukinai tendo hilo la ngono.Hata alivyoonana na Mwalimu Beatrice,mwanamke aliyemfundisha mapenzi,hakushtuka sana!Mwalimu Beatrice,akatumia kila njia ili tu aonje tena penzi la Abraham,lakini jitihada zake zilionekana kugonga mwamba.
“Kwanza nakuchukia sana Mwalimu Beatrice”
Siku hiyo Abraham,alifoka simuni.
“Kwanini Darling?”
“Usiniite Darling,mimi sio Darling wako.Mnafki wewe”
“Baby usiseme hivyo”
“Kumbe nini?Wakati ulisababisha nikafukuzwa shule,nikarudia darasa tena.Mimi ningekuwa mbali sasa hivi”
“Abraham nisamehee”
“Nishakusamehee lakini huwezi kuwa mpenzi wangu”
“Kumbuka tulipotoka”
“Sitaki kukumbuka,achana na mimi”
Alichokuwa anazungumza Abraham,kilikuwa na ukweli kabisa.Hakutaka kurudiana na Mwalimu Beatrice,alichowaza yeye ni mapenzi motomoto, aliyokuwa anapewa na Mama Maria kwani alikuwa akilelewa kama yai.Sio siri, Abraham alijisikia na alikuwa ana mikogo kuliko kawaida.
Na kilichofanya aringe zaidi ni baada ya kurudi kwa wazazi wake waliomzaa,ambao walimuonesha upendo kuliko kawaida,akazidi kudekezwa kama kifaranga cha kuku.Abraham,hakuwahi kufua tena,hakuwahi kufagia.Kila kitu alikifanya Mama yake,Marietha.Ambaye alionekana kumpenda mno!Maisha kwake yakabadilika kwa kiasi cha kutosha akawa mtoto wa Kishua.Ingawa aliishi, mbali kidogo na Mama Maria lakini mapenzi yao yaliendelea kunoga kila kukicha,hawakuweza kupitisha siku bila ya kupigiana simu ama kuchat.
“Yes Dee…Ulisema nikuone wap?”
Huo ulikuwa ni ujumbe,uliosomeka juu ya kioo cha simu ya Abraham,akiwa anachat na Mama Maria.
“Hiv upo c’riaz?”
“Yes mpenz”
“Sasa hiv usiku lakini”
“Wew niambie popote ulipo,n’takuja”
“Kweli?”
“Ndio Mpenz nakumisi”
“Hata mimi..Ukifika shule ya Azania,niambie”
“Poa”
Abraham,alimaliza kuchat na Mama Maria huku nyoka wake akiwa tayari amesimama kwani alijua kivyovyote vile Mama Maria alitaka kupewa uroda,ndiyo maana akaanza kupiga picha jinsi itakavyokuwa akikutana naye,wafanye tendo la kuzini wakiwa ndani ya gari.
Alichowaza yeye hapo ni jinsi ya kuwatoka na kuwadanganya wazazi wake.Alijua kivyovyote vile,asingeruhusiwa kutoka usiku huo!Licha ya yote,akapiga moyo konde,akavuta shati lake na kuliweka mwilini,safari ya kwenda seblen ikaanza ambapo huko alimkuta Baba yake na Mama yake, wapo juu ya makochi,wanatizama taarifa ya habari.
“Naenda kununua vocha”
Abraham,akasema huku akiwa anatembea kuufuata mlango,lakini Baba yake, Mzee Karekezi,akamzuia!
“Rudi ndani ukalale,sasa hivi usiku”
Deo Karekezi,akamwambia mwanaye.Hakutaka atoke usiku!
“Narudi sasa hivi Baba”
“Hapana rudi ndani,mtandao gani unatumia?”
“Voda”
“Nakutumia salio”
Abraham akakosa kisingizio kingine,akabaki amesimama mlangoni kama mlingoti,ameishiwa pozi.
“Mtumie mwanao salio la elfu tano.Toa kwenye Mpesa”
Deo akamwambia mkewe Marietha huku akimkabidhi simu yake,ili zoezi hilo lifanyike.
“Ngoja nikutumie,Sasa hivi usiku Abraham.Alafu wewe ni mgeni huku”
“Aya”
Abraham,aliitikia lakini moyoni aliumia,akarudi chumbani kutafakari upya!Ilikuwa ni lazima akaonane na Mama Maria siku hiyo,amdinye ndani ya gari kwani ndizi yake ilikuwa tayari imechachamaa kichupa kimejaa,hakujifikiria mara mbili!
Akanyata taratibu na kufungua mlango,akatembea kiminyato na kufungua mlango wa jikoni,akatokeza nje.Akatizama huku na kule na kutembea mpaka ukutani,niya yake ilikuwa ni kuruka ukuta atoke nje,atembee mpaka kituo cha Azania,alisubiri gari la Mama Maria.

********
Mama Maria,alikuwa juu ya kitanda.Jicho moja limemvimba uso wake mwekundu kama nyanya,umevulia damu, hiyo ni kutokana na kipondo kikali alichochezea kutoka kwa mmewe wa ndoa,ambaye muda mrefu alikuwa akimfuatilia kwa kutuma watu wake,ndiyo maana siku hiyo mchana akaingia kimyakimya kama jambazi na kuanza kumuhoji mkewe maswali yasiyokuwa na idadi kamili,picha lilionekana kuwa ni baya, baada ya Mmewe kutoa vithibitisho mbalimbali kama risiti za hoteli alizolala na mtu anayeitwa Abraham,kilichomuuma zaidi pesa zake zilikuwa zikitumiwa vibaya.Kila kitu mmewe, alikuwa nacho mpaka kopi ya tiketi aliyosafiria na kwenda jijini Mwanza mbali na hapo, aliambiwa mpaka hotel aliyofikia.
“Nikupe nini wewe Mwanamke Malaya mbwa,huyu si kama mtoto wako?”
Siku hiyo Ibra alifoka kwa hasira huku akitetemeka kwa jazba kwani alitoka kuchat na Abraham muda mfupi tu,akijifanya yeye ndiyo mama Maria.
“Nakuuliza wewe Malaya uliyekubuhuu,nikupe niniiii?Roho yangu?”
Hapo hapo akamrukia Mama Maria mithili ya Swala,akamvuta na kumdondosha chini,kilichofuata hapo kilikuwa ni kipigo kwa kwenda mbele,akamuinua kwa staili ya kuzivuta nywele zake.Mama Maria,aliachia ukelele wa maumivu lakini hiyo haikusaidia.
“Sasa leo naenda kumuuwa huyo Awara wako,mbele ya macho yako.Twende,kenge wewe”
Siku zote za Mwizi ni arobaini na arobaini ya Abraham, ilikuwa tayari imefika,kutokana na hasira chafu alizokuwa nazo mwanamme huyu aliyekuwa mwenye uchungu wa kumegewa mkewe, ilikuwa ni wazi kabisa lolote baya linaweza kutokea mbeleni.Wakatoka mpaka nje,Mama Maria akiwa analia machozi,akajuta kwa kitendo alichokuwa amekifanya nyuma.
“Ingia ndani ya gari”
“Paaaaa!”
Ulikuwa ni mlio wa kibao, kilichomfikia Mama Maria juu ya uso,kikamfanya aende mpaka chini mzima mzima puu!Mambo hayakuishia hapo,akainuliwa na kuingizwa ndani ya gari na safari ya kwenda shule ya Azania kuanza mara moja.Baba Maria,alikuwa nyuma ya usukani,anatembeza gari kwa kasi ya ajabu.Akitamani mpaka gari lipae,akiwa amefika mataa ya Ubungo,simu ya mkewe ikaita,alivyoitoa akaona jina Abraham juu ya kioo,hapohapo akaikata na kuandika ujumbe.
“Tuma meseji Love,nina drive.Npo njiani ninakuj..Lov yoh”
Baba Maria,akatuma ujumbe huo akijifanya yeye, Mama Maria!
“Okay my dear,nimekumisi.Nimemisi kifua chako,nimemisi kukushika shika,nimemisi penz lako.Nishafika nipo hapa Azania,maabuba wang..”
Baba Maria alisoma ujumbe huo kutoka kwa Abraham,ukazidi kumpandisha mori,akapandwa na usongo ajabu.Hakuelewa, angemfanya nini Abraham,endapo angemtia mikononi mwake.Taa za kijani zilivyowaka,akapiga gia na kuliondosha gari kwa hasira huku akiyabana meno yake!

*********
Laiti kama angemsikiliza Baba yake mzazi,wenda angeenda kuepuka janga analofuata.Kifupi Abraham alifanikiwa kuruka ukuta na alikuwa akienda kufuata matatizo makubwa mno,akidhani wenda aliyekuwa anachat naye muda mfupi ni Mama Maria.Tayari alikuwa amefika stendi ya mabasi shule ya Azania,anamsubiri Mama Maria kwa hali na mali kwani mawazo yake yote yalikuwa ni kufanya naye ngono,ndiyo maana kila wakati alikuwa akitizama kila gari lililokuwa linasimama stendi,dakika kumi baadaye.Marcedez benz ikapiga breki za ghafla, karibu na miguu yake,gari hiyo aliitambua sana kwani ndiyo alikuwa akiitumia Mama Maria siku zote.Akatabasamu kidogo na kulisogelea gari hilo huku akijiamini,akimsubiri Mama Maria ashuke, kama anavyofanya.Hakuelewa kama siku hiyo kwake ilikuwa ndiyo kihama!



Kilikuwa ni kitendo cha kufumba na kufumbua kwa Mme wa Mama Maria,kwani Mama Maria alifungua mlango kwa kasi na kutokeza nje!
“Abrahaam kimbiaaaa”
Hakutaka Abraham, aingie kwenye matatizo makubwa namna hiyo,kivyovyote vile aliamini yeye ndiye chanzo,ndiyo maana kama Msalaba alitaka kuubeba mwenyewe.lilikuwa ni kosa kubwa sana kwa Abraham,kubung’aa akijaribu kutafakari na kumuangalia Mama Maria, alivyoshuka ndani ya gari,kutokana na giza lililokuwepo usiku huo,haikuwa rahisi kuona majerahaa aliyokuwa nayo Mama Maria usoni,ndiyo maana aliganda kwa sekunde moja.Hapo ndipo mlango wa mbele ulipofunguliwa,akashtukia amedakwa shati,bila kuuliza chochote alipigwa kibao cha usoni kikali,kilichomuingia kisawaswa kwani ukubwa wa mkono wa Baba Maria ulitisha, ndiyo maana Abraham akahisi kama amepoteza ‘network’akaanza kuona nyota.Hakukaa sawa,akapokea kibao kingine, hiko kilimuyumbisha na kumfanya arudi kinyumenyume.Akashikwa shati!
“Leo nakuuuwa,lazima niondoke nawewe.Wewe ndio bingwa wa kutembea na wake za watu,si ndio?”
Baba Maria alizungumza kwa ukali wa hali ya juu sana,mbaya zaidi ukilinganisha na umri aliokuwa nao Abraham nayeye, vilikuwa ni vitu viwili tofauti kwani makamo ya Abraham na binti yake Maria, yalikuwa sawa,kwa maana hiyo Abraham alikuwa ni kama mtoto wake wa kumzaa.
“Nakuuwa leo,pimbi wewe!Twende ndani ya gari”
Yalikuwa ni maneno ya kutisha kutoka kwa mzee huyu mwenye hasira,ambaye alikuwa tayari amemkunja Abraham, anamvutia ndani ya gari kwa niya ya kwenda kumfanyia vitu vibaya vya kinyama.Jinsi Abraham alivyokuwa akitetemeka iliogopesha, ndiyo maana alihisi haja kubwa na ndogo kwa wakati mmoja,alijuta ni kwanini alijitokeza!Akawakumbuka wazazi wake, aliowaacha ndani,kuondoka na Baba Maria kulimaanisha kuwa wazazi wake wasingejua alipo hata kama angeuliwa!Alivyotafakari hivyo,akaogopa zaidi.Mara ghafla, wazo jipya likamjia kichwani,amtoke Baba Maria.
“Lolote na liwe,siwezi kupelekwa nisipopajua kizembe, lazima nijitetee”
Abraham aliwaza akiwa tayari amefikishwa nje ya mlango wa gari,shati lake limeshikwa vizuri amekwidwa!Kwa nguvu za ajabu,akashika vifungo vya shati lake,akavikata na kumsukumiza Baba Maria kando,akabonyea kwa chini kidogo na kumuachia Baba Maria shati,mbio alizotoa hapo zilitisha kwani alivuka barabara bila kuangalia huku na kule akiwa hana shati mwilini,alimanusura gari limgonge.
Hakutaka kusimama akakimbia mbio za kipepe!Baba Maria alivyotulia sawa,akalishika shati aliloachiwa,akasubiri magari yapite nayeye akavuka na kuanza kumkimbiza Abraham,hakujali ilikuwa ni lazima ale naye sahani moja.Kwa mara ya kwanza Abraham, alionekana mjanja lakini kwa kitendo alichokifanya alikuwa tayari ameshajiharibia kwani badala ya kuingia katikati ya mitaa ili ampoteze Baba Maria,alichofanya yeye ni kupanda ukuta wa nyumbani kwao na kuzama ndani,hakujua kwamba Baba Maria amemuona na alichofanya ni kuzunguka, mpaka upande wa geti la nyumba aliyomuona ameingia, Abraham!
“Ding dung”
Baba Maria,akabonyeza kitufe cha kengele!
“Ding Dung”
Kengele iliyobonyezwa nje,ikasikika Seblen!Deo Karekezi na Marietha walikuwa juu ya makochi, wametulia wanaangalia taarifa ya habari bado.Jambo hilo likafanya waangaliane kwani hakuna hata mmoja kati yao,aliyetegemea kupata mgeni usiku, namna hiyo.
“Ding dung”
Kengele,ikalia tena!Wa kwanza kusimama alikuwa ni Deo.
“Nani sasa hivi usiku wote huu?”
Marietha,akahoji nayeye akasimama ili kumfuata Mme wake nyuma kwani alitaka kumjua mgeni huyo ni wa aina gani.
“Baba Abraham,wasije wakawa majambazi tu”
“Baki ndani,wacha mimi niende”
“Hapana twende wote”
Deo na Marietha,wakafungua mlango na kuanza kutembea mpaka getini.Kabla ya kufungua geti,Deo akasogeza kimlango kidogo ili kujua ni nani aliyekuwa nje,anabonyeza kengele usiku huo!
“Wewe nani?Unataka nini?”
Deo,akauliza kwa ukali kidogo baada ya kumuona mzee wa Makamo,anahema jasho linamtoka kwa mbali.Hiyo ni Kutokana na taa kubwa ya Watt 80, iliyokuwa nje juu ya geti kuwa na miale mikali,ilifanya Baba Maria aonekane vizuri tu kuanzia juu utosini, mpaka chini.
“Samahani,kuna kijana ameingia humu ndani sasa hivi?”
“Hakuna kijana aliyeingia humu”
“Ameruka ukuta”
“Nimekwambia hakuna mtu,aliyeingia humu ndani”
“Shati lake hili hapa”
Baba Maria,akalishika shati vizuri,aliloachiwa na Abraham.Marietha,akawa makini kulitizama.Shati hilo la drafti, alilijuwa sana sababu ndilo alimnunulia Abraham alivyoenda Mwenge, kwenye duka la Makoba.
“Shati la Abraham hili”
Marietha,akaropoka!
“Enhee,ndio huyohuyo anaitwa Abraham”
Baba Maria,nayeye akasema!
“Mbona amelala muda mrefu sana.Wewe wa nini?Na shati lake umelitoa wapi?Nawewe ni nani?”
Marietha,akaibuka na maswali zaidi ya mawili,alitaka kujua mzee huyu anamtakia nini mtoto wake!Deo, yeye alibaki kimya anamtizama mzee huyo Baba Maria aliyekuwa nje,niya yake ilikuwa ni kusikiliza atajibu nini,ndiyo maana alikuwa makini kumtizama!
“Inabidi umuulize shati lake nimelitoa wapi”
“Wewe ndio utuambie.Kwa sababu yeye amelala tangu saa kumi na mbili na hajatoka leo siku nzima”
Marietha,akawa anajaribu kumkingia kifua, Abraham.
“Nilikuwa naye hapa sasa hivi,amenikimbia na kuniachia shati”
“Sasa hivi?!”
Deo akauliza kwa mshangao wa waziwazi.
“Ndio,nyie ni wazazi wake?”
“Ndio”
“Naomba niingie ndani,niwaambie kilichotokea.Ili tujue tunamaliza vipi hili swala zito”
“Sawa karibu”
Deo,akaongea na kuanza kufungua komea la geti!
“Baba Abraham,unamkaribisha huyu Mzee, unamjua?”
Marietha akamuuliza Deo!Alikuwa ana kila sababu ya kumuuliza, sababu alielewa kuna jambo sio zuri, litaenda kutokea.
“Itafahamika humu ndani”
“Kama jambazi je?”
Hapo Deo,akasitisha kidogo zoezi la kufungua komeo la geti na kumtizama Mkewe kwa kama sekunde tano hivi.
“Mwache tumsikilize”
Komeo likafunguliwa,Baba Maria akazama ndani.
“Karibu”
Wakaanza kutembea na kuingia ndani mpaka seblen,wote wakakaa juu ya makochi.
“Ulisema Abraham, kafanya nini?”
Deo,akamkaribisha na Swali mzee huyo, aliyeonekana kuwa na jazba kwa mbali.
“Nilikuwa naye kule Azania,sio muda mrefu”
“Azaniaaa?”
“Amenikimbia na kuniachia shati,katika kumkimbiza.Nikamuona anaruka ukuta hapo nje,nikasema ngoja niingie humu ndani”
“Ilikuwaje?”
“Anatembea na mke wangu”
Moyo wa Deo,ukapiga paa!Akamtizama Marietha kidogo na kurudisha macho yake kwa mzee huyu anayetamka maneno, mazito namna hiyo!
“Anatembea na mke wako?!”
Haikujulikana kama Deo kauliza swali,ama ameshangaa!
“Ndio,anatembea na mke wangu.Tangu muda mrefu tu,yaani leo nilikuwa nimeoneshe cha mtema kuni”
“Sio kweli”
Marietha,akabisha.Hata kama ulikuwa ni ukweli alikuwa ana kila sababu ya kumtetea mtoto wake!
“Ni kweli,subiri nikuoneshe”
Baba Maria,akatoa simu ya Mkewe na kuingia kwenye ukumbi wa meseji.Akamsogelea Deo Karekezi,Marietha hakutaka kupitwa na umbeya, nayeye akasogea karibu na kuanza kusoma meseji mbalimbali,walizokuwa wanatumiana Mama Maria na Abraham.
‘bei,umejua kunikuna.Kesho basi!Lov..Nakumisi sana,njoo uninyonye maziwa..Namisi lips zako mpenzi.Unajua sn kunifikisha….Sio siri,umejua kunikamata….Nakpenda sana Abraham wangu,tafadhali usiniache…Nakupenda sana Mpenz wangu,napenda lips zako…Nipo room no.12 njoo haraka,zimenipanda’
Hizo ndizo meseji zilizokuwa zinasomeka juu ya kioo cha simu,wakaingia kwenye ‘WatsApp’ humo ndio zilikuwa za kutisha,kilichowashangaza zaidi ni picha za nusu utupu alizokuwa, anatumiwa Abraham.Hapohapo Deo,akaangalia chini na kutingisha kichwa kwa masikitiko makubwa,akabana meno yake kwa hasira.Bila kujibu chochote, akasimama wima!
“Baba Abraham..”
Marietha,akaita baada ya kuona Mmewe, anaelekea kwenye kordo,ilikuwa ni wazi kabisa alikuwa anaenda chumba alichokuwa analala Abraham.Hakuna siku aliyochukia kama siku hiyo,ndiyo maana alitembea kwa kasi mpaka chumba cha Abraham, kilichokuwa mwisho upande wa kushoto,akakinyonga kitasa na kuzama ndani,alivyopiga jicho kitandani akamuona Abraham yupo kitandani, amefumba macho,hakutaka kujiuliza mara mbilimbili,akatafsiri moja kwa moja jambo hilo ni maigizo!
“Wewe Abraham”
Deo akaita lakini Abraham alikuwa kimya.
“Abraham,najua haujalala.Embu amka kabla sijaja hapo,nikupige mpaka nikutoe meno”
Hapo ndipo Abraham akahisi kama mkojo unataka kumpenya,ni kweli hakuwa amelala, alifumba macho yake ili kuzuga!
“Abraham amka”
Deo,akafoka kwa jazba ni wazi kabisa alikuwa tayari amepandwa na hasira.Akasogea karibu na kitanda na kumshika!
“Abrahaaam..”
“Naam Baba”
“Njoo seblen haraka sana”
Sura ya Deo ilitisha,Abraham hakuwahi kumuona baba yake akiwa katika hali kama hiyo!Siku zote, alikuwa katika tabasamu,ndiyo maana alitetemeka lakini akajitoa kitandani taratibu,akavuta fulana iliyokuwa karibu na kuiweka mwilini,wasiwasi wake ulikuwa ni juu ya Baba Maria.Lakini hakuwa ana uhakika kama Baba Maria alifika nyumbani hapo sababu alikuwa chumbani amejifungia wala hakusikia, anavyoingia ndani.Alichofanya Abraham ni kutoka akiwa na wasiwasi mkubwa,alivyotokeza seblen ndiyo kabisa,akahisi kama nguo yake ya ndani imelowana hakujua kama ni mkojo ama jasho!Hiyo ni baada ya kumuona Baba Maria,amevimba kwa hasira kama chura!
“Unamfahamu huyu?”
Deo,akamdaka na swali.
“Nakuuliza,unamfahamu huyu mzee?”
Abraham,akabaki kimya!
“Nakuuliza kwa mara nyingine.Unamfahamu huyu mzee?”
Abraham,alikuwa amesimama wima anamtizama Baba yake alivyokuwa amekunja sura kwa hasira macho mekundu,hakuelewa ni kitu gani akijibu japokuwa alikuwa anamjua Baba Maria,lakini alijuwa kabisa akijibu ‘ndio’ angeulizwa swali lingine.Umemfahamu vipi?Ndio maana akili yake ikafanya kazi kwa kasi ya roketi.
“Hapana sim…..”
“Paaaaa!”
Kilikuwa ni kibao alichopigwa Abraham na Baba yake,akayumba na kujigonga kwenye ukuta.
“Unamfahamu huyu mzee?”
Mambo yalikuwa sio Mambo,Marietha akasimama kwa niya ya kumshika Deo ili asimpige, Abraham.
“Unamfahamu huyu Mzee?Abraham.Nitakupiga nikupasue,hivi hunijui vizuri mimi”
Marietha, alimjua sana Mmewe akiwa ana hasira,ndiyo maana hata yeye alianza kuogopa,kulikuwa kuna kila dalili mbaya ya Abraham kushushiwa kipigo cha 4G siku hiyo!
“Abraham mwanangu sema ukweli”
Marietha,akaingilia kati lakini alifanya hivyo huku akiwa amekaa mbele ya Deo ili kumkingia kifua Abraham kwani upepo haukuwa mzuri usiku huo!
“Abraham,nijibu swali langu”
Deo akataka kujibiwa swali,ndiyo maana akatoa kichwa chake na kumchungulia Abraham kwani mbele yake alisimama Marietha.
“Ninamfahamu ndio”
Hatimaye, Abraham akajibu kwa hofu.
“Unamfahamu, vipi?”
Deo,akaibua tena swali.
“Unamfahamu vipi nakuuliza?”
“Ni ni ni ninini ni jirani yetu kule tulipokuwa tunaishi Kawe”
“Una uhakika?”
“Ndio Baba”
Deo,akamsogelea Baba Maria na kuchukua shati la Abraham,alilokuja nalo.
“Hili shati ni lako,uliliacha wapi?”
Abraham,akalitizama shati lake!Hakujuwa ni jibu gani alitoe,swala ni kwamba alijuwa kila kitu.Akaanza kutafakari.
“Nijibu swali,hili shati uliliacha wapi?”
Deo alitaka jibu,ndio maana akakomaa na swali lake.
“Baba nisamehee”
“Hilo sio jibu”
“Naomba nisamehee”
“Kwa kosa gani?”
Deo,alikuwa akitetemeka kwa hasira kama mtu mwenye homa ya usiku,hiyo ilimuogopesha hadi Marietha lakini ilikuwa kama Mama ni lazima amtetee mwanaye kwani alielewa siku hiyo kipondo chake kisingekuwa cha kawaida.
“Babaa lakini Mi…”
“Abraham,nitakupiga nikafungwe tena, ujuwe!Nani anakufundisha kutembea na wanawake waliokuzidi umri?Nani kakufundisha huo umalaya?”
“Baba Abraham,tukae chini.Tuzungumze ili tujue tunamaliza vipi hili swala”Marietha,akasema.
“Kaa pembeni kwanza.Unajua maana yake?Angekufa je?Unajua kesi ya mke wa mtu wewe?”
Deo,akamsogeza Marietha pembeni,akitumia nguvu.Kwa kasi ya mwewe, Deo akachomoa mkanda kutoka kwenye suruali yake,hapohapo akaanza kumchalaza Abraham kila sehemu ya mwili wake,alivyotaka kukimbia akashikwa mkono, hapo ndipo Deo hasira zilimpanda zaidi,akaanza kumpiga makofi ya uso!
“Baba Abraham utamuua Mtoto,Baba Abraham achaaa”
Marietha,akasema huku akijaribu kumvuta Deo,lakini ikashindikana, Deo akazidi kutembeza kipondo.Hakujali maumivu aliyokuwa anapata Abraham,kibao kimoja kilimpata Abraham usoni,alikuwa mbele ya ukuta.Kichwa chake kikajipigiza ukutani,hapohapo akadondoka chini na ukimya wa ghafla ukaibuka,Abraham akawa ametulia.
“Abrahaam”
Marietha akaita,akachuchumaa chini.
“Abraham”
Akaita huku akimtingisha lakini Abraham,hakutingishika!Hiyo ilimfanya apatwe na hofu zaidi,akaweka mkono wake puani kwa Abraha ili kusikilizia kama hewa inatoka.
“Abrahaaaaaaaaaam!”
Marietha,akaachia ukelele baada ya kuona hakuna hewa inayopita puani,kumaanisha kwamba.Abraham hakuwa na uhai,ameaga dunia!



Marietha yupo chini,anahisi kama uti wake wa mgongo umepigwa na ubaridi mkali.Moyo wake unamdunda kwa hofu kubwa, hiyo ni baada ya mwanaye kipenzi kupigwa mpaka kudondoka chini,mbaya zaidi hakuwa anahema wala kujigusa, kumaanisha kwamba mapigo ya moyo yamesimama.Jambo hilo lilimfanya apige yowe huku akiwa chini amemkumbatia mtoto wake,analia kwa sauti huku akimtupia lawama Deo kwani ndiye aliyekuwa mkandarasi wa hayo yote kutokea.
“Deooo,Umeniuliaa mwanaanguuuuu!Uwiiiiiii”
Marietha alikuwa akipiga yowe la nguvu,huku akimtingisha Abraham, ambaye alikuwa kimya kabisa.Hiyo, ilimfanya Deo aanze kutetemeka akaamini hasira ni hasara siku zote!Baba Maria, nayeye ikambidi asimame kutoka juu ya kochi,atizame chini hata yeye aliogopa.Kwani kulikuwa kuna kila dalili ya kifo cha Abraham.Bila kujifikiria Deo akapiga moyo konde na kukimbia mpaka chumbani ambapo huko alikwapua,rimoti ya gari,alivyofika seblen akamuinua Abraham na kumbeba, haraka wakatoka nje huku nyuma Marietha na Baba Maria,wakimfuata nyumanyuma.
“Twii twiii”
Kelele za gari baada ya Deo kuminya Rimoti ikasikika,akauparamia mlango wa nyuma na kumuingiza Abraham ndani ya gari,Marietha akazama ndani kama Mwanajeshi.Baba Maria hakujua afanye nini lakini nayeye, alijikuta anaingia ndani ya gari bila kuambiwa!Gari la Deo kwa ndani lilikuwa na rimoti inayofungua geti,akabonyeza rimoti, geti likaanza kufunguka,akapiga gari ‘rivasi’akiwa amekanyaga mafuta mengi,shingo yake ameigeuza nyuma,kwa mwendo aliotoka nao ilifanya agonge geti, taa ya nyuma upande wa kushoto ikapasuka hapohapo,hakujali.Alivyolitoa gari nje,akaweka mguu kati na kuzungusha usukani, akakanyaga mafuta mengi.Mwendo, aliotoka nao hapo,uliogopesha!Hakutofautishwa na jambazi, aliyetoka kuvamia benki,uzuri wa eneo analoishi na hospitali ya taifa Ya Muhimbili,ukaribu wake ulikuwa ni sawa na pua na mdomo!Akanyoosha moja kwa moja,kilichomchanganya akili zaidi ni kelele alizokuwa anapiga Marietha ndani ya gari,akimtupia lawama yeye!Hiyo ilimfanya akanyage mafuta zaidi huku akiwa anasali Abraham asife kwani aliamini yeye ndiye angekuwa muuaji na kwa kosa hilo,asingejisamehee hata kidogo kwa kumuuwa mwanaye kipenzi kwa mikono yake!Alitamani masaa yarudi nyuma abadilishe kila kitu kilichotokea lakini haikuwezekana,ukweli ulikuwa ni kwamba Abraham ana hali mbaya ya kutisha!Dakika nne baadaye walikuwa nje ya lango la Hospitali ya Taifa, Muhimbili!Deo akaliingiza gari ndani.Kabla hajapaki vizuri akateremka bila hata kufunga mlango wa gari.
“Nesiiii,msaaadaaa”
Deo,aliita akipunga mkono juu huku akikimbia kuelekea mapokezi.Wauguzi wa hospitali hiyo walikuwa makini,walivyoona hivyo wakajua kuna jambo la dharura.
“Wapi?”
Nesi mmoja akamvaa na kumuuliza.
“Kwenye gari yangu ile pale”
Manesi wakaanza kulifuata gari kwa kasi,wakafungua mlango.Haraka, machela ikasogezwa Abraham akawekwa juu yake,ikaanza kukimbizwa mkuku mkuku.Marietha akawa anaikimbilia huku analia machozi.
“Abraaaaham wangu,usifee mwanangu.Bado nakupenda…Ehhh Mungu Weee!”
Marietha alikuwa akipiga yowe huku akibubujikwa na machozi,kamasi zinamtoka!Deo japokuwa alikuwa ni mwanamme lakini hata yeye alionekana kama mwehu,hakuelewa ni kitu gani akifanye!
“Naomba msubiri hapa”
Deo na Marietha wakazuiwa,ilielekea chumba hiko hakiruhusiwi kuingia mtu, isipokuwa mgonjwa ama wauguzi tu.
“Deoooo,Kwaaniniii lakiniii,unge….msikilizaa japo kidog..o kwanini Umemuuwa Abra..ham?”
Kwa Marietha,alihitimisha moja kwa moja na kukata tamaa!Tayari alishaamini ya kuwa Abraham amefariki Dunia, ndiyo maana akaanza kumtupia lawama Mmewe.
“Mke wangu.Mungu ni mkubwa”
“No no noo Hapaaana,usinishikeee”
Kila kitu kilionekana kuharibika na Marietha alionekana kama mwanamke aliyekata tamaa ya mwanaye kupona,alikuwa mwenye kila sababu ya kuamini hivyo, sababu alivyokumbuka yakuwa Abraham hatoi hewa yoyote ile, ndiyo ikamuumiza zaidi.Deo kama mwanamme, akavaa jukumu la Mume,akamsogelea Marietha na kumkumbatia kwa nguvu akijaribu kumpa moyo.Lakini kwa Marietha ilikuwa ni sawa na Kumpa mifupa atafune kibogoyo!Kwake yeye alilia tu ingawa mumewe alijitahidi kumbembeleza na kumwambia kuwa kila kitu kipo sawa,amsemehee!
“Kwanini umem..piga?”
Marietha akauliza kwa kwikwi,akiwa kifuani mwa Deo analia machozi.
“Ni hasira tu”
“Ndi..o umpige kama mwiz..i?”
Kazi ya Deo ikawa kama inaanza kuzaa matunda,kwani Marietha taratibu alianza kuelewa na kutulia.
“Atapona?”
Marietha,akahoji kitu ambacho hakikuwa na jibu, kwani mpaka muda huo hakuna hata daktari aliyetokeza!
“Ndio,atapona”
Deo,akamfariji.Hapo walikaa kwa takribani dakika tano nzima,ndipo mlango alioingizwa Abraham ukafunguliwa,akatokeza daktari.Wote wakamuendea kwa kasi, mpaka karibu yake!
“Dokta vipi?”
Deo,akawa wa kwanza kuhoji.
“Mwanangu anaendeleaje?Niambie ukweli”
Marietha nayeye akaibuka na swali,Dokta akashindwa aanze kulijibu swali gani, sababu wote walimtizama machoni.
“Vitu vyake hivi hapa”
Dokta,akazungumza na kuwakibidhi simu na wallet ya Abraham.Kwa Marietha jambo hilo akalitafsiri moja kwa moja kama kuna msiba tayari, kwani taa nyekundu ilianza kuwaka ndani ya kichwa chake!
“Abraaaaahaaaaaam!”
Akaanza kupiga yowe tena na kumshika daktari koti huku akianza kumvuta na kumtikisa tikisa!
“Mama utanichania koti langu!Mwanao ana hali nzuri”
Hatimaye daktari akazungumza,haikujulikana kama ana wapa moyo na matumaini ama la!Lakini akajitahidi kuwafariji kwa kuwaambia, Abraham yupo sawa na mpaka dakika hiyo wanavyozungumza,yupo katika uangalizi wa hali ya juu sana!
“Bahati nzuri,mmemuwahisha hospitali.Mapigo yake ya moyo yalikuwa yameshuka sana”
“Kwahiyo atapona?”
“Ndio,tuombe Mungu.Niacheni kidogo nirudi”
Mpaka hapo daktari,akarudi ndani ya wodi aliloingizwa Abraham,ambapo huko aliungana na wenzake saba,wakawa wamemzunguka Abraham, aliyekuwa juu ya kitanda,wanamkarabati.
Siku hiyo ikakatika na hali ya Abraham ikaonekana kuwa nzuri ya kuridhisha lakini hakuruhusiwa kuondoka hospitalini.

*******
Siku zote maumivu ya mapenzi hayawezi kufananishwa na kitu chochote kile,hasa ukipenda usipopendwa!Kila kukicha Karishma alimuwaza Abraham,chakula kikawa hakishuki,akakosa raha ya maisha!Akawa kama teja aliyepata ugonjwa mbaya wa arosto,kilichomuumiza zaidi ni majibu aliyopewa mara ya mwisho!
Hakuweza kurudi tena katika hali ya kawaida,akajitahidi kuwa bize,kuangalia ‘movie’ ili walau amsahau Abraham na amuondoe kichwani kwake lakini wapi,ilikuwa ndiyo kwanza anazidi kuchochea kuni.Karishma hakutofautishwa na kinda la ndege, lilioachwa na mama yake,moyo wake uliuma alitamani walau angekuwa na Abraham karibu yake,lakini jambo hilo halikuwezekana hata kidogo,akabaki na maumivu yake moyoni!Kilichomfanya azidi kudata ni kutoona ujumbe wowote ule wala simu ikipigwa kutoka kwa Abraham,kama alivyozoea siku zote.
“Acha leo nimpigie,kwani nina kasoro gani?Au mimi mbaya.Haiwezekani,wanaume wengi wananitaka kimapenzi”
Karishma aliongea na kujijibu mwenyewe,hapohapo akajitosa kimasomaso na kuchukua simu yake,akitaka kumtafuta Abraham hewani lakini matokeo yake iliita bila kupokelewa,ikaita tena na tena bila kupokelewa.
“Abrahaaam”
Tayari machozi yalikuwa yanaanza kumlenga,akashindwa kujizuia na kuanza kulia kabisa!Siku hiyo alishindwa kufanya kitu chochote kile,siku iliyofuata ilikuwa hivyohivyo pia!Akajaribu namba za Abraham lakini mambo yalikuwa ni yaleyale,iliita bila kupokelewa!Hapo ndipo akaamua kuingia ‘WatsApp’ na kuanza kumtumia, meseji.
‘Pokea simu zangu.Y are u Doing this to me?Is it b'coz ilove u?’
Akatuma ujumbe huo na mwishoni akaweka ‘emoji’ ya kimdoli kinachotia huruma,zilivyopita dakika mbili akaona hakuna majibu, akatuma tena ujumbe mwingine.
‘Abraham,ilove you.Nateseka kwa ajili yako!Tafadhali pokea simu zangu,japo nisikie sauti yako, Love!Au kukupenda imekuwa makosa’
Akarusha tena meseji,siku hiyo aliandika meseji zisizopungua thelathini lakini zote hazikuwa na majibu yoyote yale!Hakukoma,siku iliyofuata asubuhi sana akapiga simu.Moyo wake ukapiga kwa nguvu, hiyo ni baada ya kukuta namba hazipatikani,hapo ndipo akachoka zaidi.
Akashindwa cha kufanya,siku hiyo akakosa kabisa raha ya maisha!Siku hiyo ndiyo alishindwa kabisa kuweka kitu chochote mdomoni,akakosa hamu ya kula wala kufanya kitu chochote kile.Zilikuwa zimebaki wiki mbili tu ili likizo yake iishe na arudi chuo,hiyo ilimaanisha kurudi kwake masomoni nchini Sweden, ingekuwa ndiyo mwisho wa kuonana na Abraham,hakutaka jambo hilo litokee, ndiyo maana alikuwa akijaribu namba ya Abraham,asubuhi,mchana na jioni.Kila kukicha alikuwa akiijaribu tu, bila kuchoka!
“Au,sio fungu langu”
Karishma akajiuliza,alihisi kuchoka na kudhani wenda Abraham sio fungu lake,ndiyo maana akahitimisha kwa kusema maneno hayo!
“Abraham nakupenda,lakini nitajitahidi nikusahau tu!Ipo siku tutakutana Mungu akipenda”
Karishma siku hiyo alikuwa anazungumza maneno hayo huku akitoa laini ndani ya simu yake,akafuta namba ya Abraham na kubadili laini kabisa,kwa maana nyingine hakutaka tena kumuweka Abraham ndani ya kichwa chake akiamini kwamba kumpata Abraham ilikuwa ni sawa na kusubiri meli uwanja wa ndege!Hayo ndiyo maamuzi magumu aliyochukuwa Karishma ili maisha yake yaendelee.

*********
Ugomvi wa Issa na Katrina ulikuwa ni mkubwa sana,Katrina alikataa kukubali msamahaa.Njama za mauaji alizotaka kufanya Issa, yalifanya Katrina aogope na kutaka talaka yake mara moja.Hilo linakuwa gumu kwa Issa kwani aliomba msamahaa lakini Kwa Katrina ilionekana kuwa vigumu,sababu mambo yalikuwa tayari yameenda mahakamani ili wagawane mali na kila mtu afe na chake na awe na maisha yake!Hilo ndilo suluisho alilochukuwa mwanamke huyu wa kihindi.Na ilikuwa wazi kwamba,akishachukuwa maamuzi,ilikuwa vigumu kuyapindisha!Ndiyo maana Issa alikuwa akihangaika kwenye simu kila siku kumtafuta hewani lakini jambo hilo halikufua dafu kwani Katrina,alikuwa akikata simu na wakati mwingine hapokei kabisa!
“Issa,usinipigie simu tafadhali.Nenda kasaini mahakamani unipe talaka yangu,ni jambo dogo tu”
Katrina,alihitimisha simuni siku hiyo, baada ya kuita kwa muda mrefu.Alifanya hivyo ili kutoa kero!
“Katrina,tukae tuongee!Haina haja ya kufika huko”
“Siwezi kuishi na jambazi mimi,ipo siku utakuja kuniua”
“Lakini Ka…”
“Lakini nini?Lakini nini eeeh?Nimekwambia kasaini barua ya talaka tuachane”
“Mtoto atalea nani?”
“Karishma keshakuwa mtu mzima,mpaka alipo anaweza kujitegemea pia bila baba”
“Katrina”
“Issa,kasaini barua mahakamani.Ili nikachukuwe separate sheet,siwezi kuishi na mwanamme kama wewe nishasema,nimekuvumilia mengi sana.Sasa yatosha”
Katrina alizungumza maneno hayo kwa jazba nyingi,akiwa juu ya kochi seblen bila kuelewa Karishma yupo,kwenye pembe ukutani anasikia kila kitu.Hapo ndipo alipogundua siri hiyo nzito, kuhusu wazazi wake!
“Mooom!”
Karishma akaibuka,seblen.Akiwa mwenye jazba tele, ukichanganya na mawazo na ‘stress’ za kumkosa Abraham,ikamfanya apate sehemu ya kuzitua, hasira zake!
“Kwanini unakuwa muongo?Uliniambia Dad amesafiri?Kwanini lakini?”
Karishma akauliza kwa sauti ya juu,nayeye akaibua sekeseke kwa mama yake!
“Nataka kuonana na Dad,sasa hivi.Najua hajasafiri,mnataka kuachana.I don’t like it na ukimuacha Dad,Count me out”
Karishma alizungumza akimaanisha, tena kwa hasira za waziwazi,hiyo ilimfanya Mama yake aishiwe pozi,akashindwa kujibu kwani hakuwahi kumuona Karishma akiwa katika hali kama hiyo!
“Karishma My daughter,you should calm down first”(Karishma binti yangu,ungepunguza jazba kwanza)
“No,Those are my terms, Mama.I don’t care”(Hiyo ndiyo misimamo yangu Mama,sijali)
Karishma alivyomaliza kuzungumza hivyo,akaingia chumbani ambapo huko Mama yake alimfuata na kumbembeleza, apunguze hasira na kumuhaidi kuwa, Baba yake atarudi nyumbani siku moja.
“Lini?”
“Tumepishana tu kidogo,lakini atarudi”
“Atarudi wakati nimesikia,you need a divorce!I’m not a kid”
Karishma alikuwa tayari anajielewa,alijuwa nini maana ya talaka na ndiyo maana hakutaka jambo hilo litokee.
“Karishma lakini ungenisikiliza,wewe ni mtoto bado”
“Mama,naomba uniache.Ukiachana na Dad,mimi sitokuwa tena mwanao.Nape..nda wazazi wangu muwe pamoja,pleas..e nakuomba”
Hapo Karishma akaongea huku sauti yake ikikwaruzika,ni dhahiri kuwa alikuwa tayari anaanza kulia machozi,akitaka wazazi wake wasitengane.Jambo hilo lilimuuma sana Karishma,hatimaye akasimama na kuelekea seblen,hapohapo akachukuwa simu na kumtafuta Issa,hewani!
“Issa….Sawa nimekubali ombi lako.Lakini kwa sharti moja tu”
Dokta Katrina,alizungumza na Issa simuni baada ya kupokelewa!
“Sharti gani?”
“Nahitaji uonane na Mr Deo Karekezi,mkae chini.Myaweke sawa!”



Kitendo cha Katrina kuzungumza maneno hayo,ukimya wa ghafla ukatokea!
“Halloo,Issa.Umenisikia?”
Katrina ikabidi asisitize.
“Ndio nimekusikia”
“Upo tayari lini?”
“Hata Kesho,nakupenda Katrina.Sina jinsi”
“Ahsante,Kesho nitakutafuta”
Isingekuwa mtoto wake wa pekee, hata siku moja asingeweza kurudisha moyo wake nyuma na kurudiana na Issa,ambaye kwake tayari alimfananisha na Jambazi!Hivyo alilazimika kumtoa kabisa ndani ya moyo wake!Lakini leo hii mambo yamebadilika, akajikuta anamuhitaji tena kwani alimuhurumia sana binti yake,Karishma.
Mbali na hapo, bado alikuwa ana chembechembe za penzi la Issa, ndani ya damu yake.Usiku ulikuwa tayari mwingi,Katrina alivyotaka kumtafuta Deo Karekezi hewani,akasita sababu aliogopa kumsumbua, mbali na hapo alihofia kuvuruga ndoa kwani aliamini usiku kama huo ni muda wa wapenzi kupumzika na pia kupiga simu usiku kama huo kungeibua mtafaruku mwingine.
Ndiyo maana msomi huyu na mwelewa akawa tayari kusubiri mpaka kupambazuke ndipo amueleze kuwa anahitaji kufanya naye kikao kidogo lakini kizito!Ni kweli,kulikucha.
Kabla ya Katrina kupiga mswaki,akavuta simu yake juu ya meza na kumtafuta Deo Karekezi, hewani!
“Mr.Deo Karekezi.Habari za siku nyingi?”
Katrina alizungumza kwa uchangamfu kidogo,akitoa salam!
“Nzuri nzuri Dokta”
“Naona kimya kimezidi”
“Mihangaiko tu ya hapa na pale”
“Sasa,kuna jambo nahitaji tuzungumze”
“Jambo gani?”
“Lini una muda?”
“Nadhani baada ya siku mbili ama tatu hivi”
“Leo haitowezekana?”
“Hapana,kwa leo siwezi kuwa muongo.Haitowezekana”
“Basi,nitakupigia hiyo keshokutwa”
“Aya”
Deo,hata ingekuwa nini.Asingeweza kuchomoka hospitalini kwani alikuwa akimuuguza Mwanaye Abraham!Ilikuwa ni lazima akeshe wodini,akijaribu kuwa naye karibu ili afute kila kitu kilichotokea!Uzuri,madaktari walipambana na hali ya Abraham na iliridhisha sababu aliweza kufumbua macho na kuongea kwa mbali ingawa bado alilalamika ana maumivu ya kichwani.
“Ndio Mama,kwa huku nyuma kinauma bado”
Abraham,alizungumza akiwa juu ya kitanda cha wagonjwa!Kandokando yake, upande wa kulia alisimama Mama yake,kushoto Baba yake!
“Utapona tu mwanangu”
Mama alizidi kumfariji Mwana.
“Pole Abraham”
Deo,nayeye akampa pole mwanaye.Iliitikiwa lakini Abraham, hakumgeukia badala yake, aliendelea kumwangalia Mama yake tu,tayari alianza kumchukulia Baba yake kama katili,ambaye hana huruma.Jioni ya siku hiyo akaandikiwa dawa nyingine za maumivu,alivyodamka siku iliyofuata.
Hali yake ikawa nzuri kabisa!Hapo, hawakuwa na sababu tena ya kubaki hospitalini,wakaruhusiwa.

*******
Deo Karekezi,akavaa kazi nyingine.Kwa kitendo alichokifanya ilibidi awe karibu sana na Abraham,ndiyo maana walivyofika nyumbani tu,alitaka waende kuzurura sehemu tofautitofauti,ili kumrudisha Abraham katika akili yake ya kawaida,alitaka Abraham ampende na asahau yaliyopita ndiyo maana siku hiyo wakafunga safari na kwenda Miami Pub ili wakale, kuku kwa mrija!
“Nataka mguu wa mbuzi ulioshiba,hii nyama siitaki”
Deo Karekezi,alikuwa jikoni anakagua nyama ya kuchoma ili akale na familia yake.
“Hii sehemu nzuri mzee wangu.Ina steki”
Mchoma nyama,akasifia nyama zake huku akimuonesha Mteja wake.
“Nimekwambia hiyo siitaki.Nipe hiyo nyingine changanya na mbavu.Weka na ndizi kumi na mbili”
“Sawa mzee,tupime ya shilingi ngapi?”
“Thelathini”
“Sawa,dakika kumi itakuwa tayari”
Deo alivyorudi kwenye meza ya akina Marietha,akamuuliza Abraham kama anatumia kinywaji chochote kile.
“Sprite”
Abraham akajibu!
“Mama Abraham”
“Red Wine”
Dakika mbili zikawa nyingi,vinywaji vikawa mezani.Kama kawaida ya Deo ukiwa naye ni lazima utabasamu,hapo alianza stori.Za hapa na pale,uchangamfu wake ukamfanya Marietha aanze kucheka, mara Abraham nayeye akatabasamu,wote wakajikuta wamesahau yaliyopita,mbuzi alivyoletwa,wakanawa mikono,kuanzia hapo hakuna hata mmoja wao,aliyemuongelesha mwenzake kwani kila mmoja, alipambana na mnofu wake.Bata,halikuishia hapo!
Siku iliyofuata Abraham alizungushwa sehemu nyingi tofauti tofauti za starehe!
“Baba umepajuaje huku?”
Siku hiyo Abraham,alimuuliza Baba yake, walivyofika Blue Pearl Garden,Ubungo Plaza.
“Zamani nilikuwa nafanya kazi na mzee mmoja hapo Ubungo plaza,kipindi hiko nina maduka ya spea”
“Kwani ulikuwa una maduka ya spea?”
“Ndio,Hardwares na vifaa vya magari pia”
“Sasa viko wapi?”
“Ni stori ndefu kidogo.Lakini kifupi kwa sasa hivi, sijihusishi na hiyo biashara”
“Sasa hivi unafanya kazi gani?”
“Nipo kwenye kilimo sanasana,inabidi siku nikupeleke Bukoba wewe na Mama yako,mkaone”
“Sawa Baba”
Siku hiyo Abraham,aliibuka na maswali mengi sana!Na Deo aliyajibu huku akitabasamu kuashiria kwamba hakuna kitu chochote kilichoharibika.Maisha yakawa yanaendelea kama kawaida,Abraham akaonekana kuwa mwenye furaha kuwa na wazazi wake wote wawili.
Mbali na kufurahia na familia yake,lakini Deo alikuwa mtu makini sana kwenye biashara zake,ilikuwa kila asubuhi ni lazima apige simu,kuulizia Mafuso yake yapo wapi na alivyokata simu alipiga shambani mkoani Bukoba, kuulizia mazao yanaendeleaje!Hata hivyo hakukoma na hakuridhika kuwa na mali alizokuwa nazo,alitaka kuziongeza, ndiyo maana kila kukicha alikuwa akijaribu kutuma barua za kuomba tenda,katika shule mbalimbali!
“Ndio,unga upo..Matunda pia ninayo.Hata ukitaka gunia mia zinapatikana…Tuma Quotation,kwenye email.Ahsante sana nitashukuru,Ubarikiwe”
Deo siku hiyo alikuwa akiongea kwenye simu na mkurugenzi wa shule, zilizokuwa zinatingisha Tanzania nzima,Mama Getrude Rwakatale!Anayemiliki shule za St.Marry’s na miradi mingine mingi,ni kweli siku hiyo Quotation ikaingia ndani ya email yake na kazi yake ilikuwa ni kujaza nafasi zilizoachwa wazi,yeye akaweka bei kisha kurudisha majibu ili baadaye asubiri tenda hiyo, ambayo jumla yake alivyopiga hesabu ilikuwa ni shilingi milioni sabini na tano!Saa kumi ya jioni siku hiyo,akapokea simu tena kutoka kwa Dokta Katrina,akisisitiza kikao chake!
“Kikao hiko kinahusu nini?”
“Kwanza nataka kukulipa deni lako,alafu kingine.Mme wangu ana mazungumzo nawewe”
Dokta Katrina,akaweka mambo wazi akiwa simuni.
“Saa ngapi?”
“Leo saa moja jioni,tafadhali nakuomba”
“Wapi?”
“New Africa Hotel”
“Lakini,nitakuja na mke wangu”
“Tena, itakuwa vizuri ukija naye”
“Sawa”
Deo,alivyokata simu siku hiyo.Akasimama na kuingia chumbani.Siku hiyo hakuenda popote na Marietha alikuwa chumbani,akampasha kila kitu kilichotakiwa kufanyika,akimwambia kwamba Katrina ana mazungumzo nayeye!
“Yule Muhindi?”
Haikujulikana kama Marietha,aliuliza ama alishtuka.Sababu akili yake moja kwa moja ilimpeleka kwa Issa!Kwani alimfahamu fika muhindi huyo.
“Ndio”
“Amesema uwende namimi?”
“Nilimwambia lazima niwe nawewe”
“Aya,saa ngapi?”
“Saa kumi na mbili”
Kikao kilitakiwa kianze saa moja,Deo alisema saa kumi na mbili sababu alimjuwa mke wake, akiingia kwenye kioo kubanduka ni baada ya nusu saa!Ndiyo maana akavuta muda nyuma ili wasichelewe na asionekane mswahili.Saa kumi na moja nusu Marietha,alizama bafuni kuoga,baada ya kutoka akatafuta gauni lake zuri na jipya,akalivaa vizuri.Akakaa juu ya meza iliyojaa vipodozi vingi!Hapo ndipo muda wake mwingi, huliwa.
“Wewe mbona hujiandai?”
Marietha akamuuliza mumewe baada ya kumuona ndiyo kwanza yupo kitandani anachezea ‘laptop’
“Mimi si naingia kuoga tu”
“Huvai?”
“Nitavaa”
“Nguo gani?”
“Suti”
“Sawa,amka basi ukaoge.Tutachelewa”
“Hatuwezi”
Kwa Deo,alikuwa anajua kitu anachokifanya, ndiyo maana hakuwa mwenye presha yoyote ile.Marietha alivyomaliza kujipara,yeye akazima ‘laptop’ na kuvaa taulo,akaoga,akatoka na kuanza kuvaa!Tayari ilikuwa imegonga saa kumi na mbili na dakika saba,ndipo walipoingia ndani ya gari.
“Abraham,tunarudi sasa hivi.Akigonga mtu yoyote Yule usifungue.Kuhusu simu yako nitakutafutia nyingine”
Hayo yalikuwa maagizo kutoka kwa Marietha huku akiwa anaingia ndani ya gari,safari ya kwenda New Africa Hotel,ikaanza hapohapo!Kichaka cha Deo kilikuwa Dar es salaam, vichochoro vyote vya mji huo alivijua,ndiyo maana alipita njia za panya.Mara ghafla wakaibuka Maktaba ya taifa,wakasubiri mataa yaruhusu, wakunje ili kuifika hoteli hiyo.Wakiwa katika mataa,simu ya Deo ikaita.Aliyekuwa anapiga sio mtu mwingine bali ni Dokta Katrina,akiwataarifu kuwa tayari, amefika na anawasubiri.
“Tuko maktaba hapa,hata sisi tumeshafika”
“Ahsante kwa kuwahi”
“Usijali”
Ukweli ulikuwa huo,dakika tano baadaye Deo alikuwa ana hangaika kuegesha gari lake nje ya hotel hiyo ya kifahari,alivyoona gari ya Dokta Katrina BMW X6,nayeye akaweka gari lake kandokando yake!Akashuka,Marietha nayeye akateremka!
“Tupite huku Mke wangu”
Deo,akatoa pendekezo!Kisha kumshika mkewe mkono,wakaingia mpaka ndani ambapo huko walianza kuangaza huku na kule,Deo akaona anapungiwa mkono na Katrina!Akaanza kusogea kuelekea upande wa mwisho kabisa,ambapo huko alimkuta Issa amekaa,wakaangaliana kwa kitambo kidogo!
“Mmependeza sana”
Dokta Katrina,akamwaga sifa baada ya Deo na Marietha kuwasogelea karibu kabisa,wakapeana mikono kisha kukaa kwenye viti.
“Karibuni”
“Ahsante”
Macho ya Marietha yalituwa kwa Issa,hapohapo akakunja uso!Hakuelewa kwanini anafanya hivyo lakini moyoni mwake, alihisi uchungu ajabu,akamsogelea karibu Deo na kumshika mkono wake,kwa staili ya kumpapasa papasa alifanya hivyo makusudi,ili kumtia wivu Issa!
“Mimi na mme wangu,hatukupata muda muafaka wa kukutana, baada ya matatizo ya hapa na pale kutokea!Hivyo,leo hii naomba tuweke tofauti zetu kando ili maisha yaendelee”
Dokta Katrina, aliongea kwa sauti ya upole huku akiwatizama Deo na Marietha kwa zamu!

Alikuwa ana kila sababu ya kuomba radhi kwa yote yaliyotokea nyuma,kwani aliamini ya nyuma si ndwele!Issa alikuwa amenyamaza kimya kabisa,hana neno la kusema,anamtizama Deo!Ghafla akakumbuka mateso aliyopitia na mambo aliyofanyiwa na Deo,akamkata jicho kali Marietha,Mwanamke aliyekuwa na ndoto naye miaka mingi iliyopita lakini Deo,akaja kumpora, tonge mdomoni!
“Issa!Sikukwambia kitu kimoja,Deo sasa hivi nafanya naye biashara,ni mchapakazi sana!Sasa hivi amehamia kwenye kilimo,nimependa kumuita hapa ili mmalize tofauti zenu”
Dokta Katrina, akamaliza na kumtizama Issa,ambaye bado alishindwa kujua ni kitu gani akizungumze!Deo Karekezi nayeye, alikuwa amepiga kimya,Marietha amebenua mdomo,kuna kitu kilikuwa kimemkaba kohoni!
“Deo kwanini tupo hapa?Embu,tuwekane wazi”
Marietha,akajikuta ameropoka!
“Ngoja Marietha”
“Sio ningoje,ningejuwa kama nakuja kukutana na huyu Mwanamme nisingekuja.Haki ya Mungu tena”
Marietha,akawa tayari ametibuka!Anaropoka tu,hovyohovyo,Katrina alivyoona mambo yameharibika akajaribu kumtuliza Marietha, ndiyo kwanza alikuwa kama anatibua mambo!
“Nawewe nyamaza,huwezi kunituliza”
“Marietha,punguza jazba”
Deo,akaingilia kati!
“Sio hivyo Deo,lazima niongee kile nachojisikia”
Marietha,akawaka sio kitoto na hakuonesha ustaarabu hata kidogo!
“Nakuuliza Deo,umekuja kunileta hapa nije kuonana na Issa?”
Marietha,akabwatuka tena!
“Deo,Mwambie mkeo awe mstaarabu”
Dokta Katrina,akamwambia Deo!Amtulize Mkewe kwani tayari alikuwa anaanza kutia aibu na watu walikuwa wakiangalia meza yao!
“Marietha tulia”
“Siwezi kutulia Deo”
“Au bado unampenda Issa?Kuwa mkweli ili Mumeo ajuwe,nikuache uwe naye.Sio unaropoka.Tumekuja hapa kujenga, sio kubomoa!Tatizo lako ni kitu gani?”
Katrina nayeye akaanza kutoa povu,alishindwa kumvumilia Marietha,nayeye akapaza sauti kwani tayari alikuwa ametibuka sio mchezo!
“Nimemuita Mumeo Deo ili tuje tuyajenge hapa”
“Kwahiyo?”
“Nyamaza,tuyamalize!”
Marietha na Dokta Katrina,wakawa tayari wamepandishiana, ikabidi Deo aingilie kati na kuwatuliza!Hapo ndipo walipopoa na kutulia.Katrina,ikabidi aanze kuzungumza dhumuni na kiini cha mkutano huo mdogo ambao alitaka Deo na Issa wapatane,hicho ndicho kilichotokea kwa muda huo!
“Peaneni mikono,hii ligi iishe Issa”
Katrina akashauri,Deo na Issa wakabaki wanatizamana kama mabeberu.Kwa Deo hakuwa na tatizo lolote lile,akatoa mkono na kumpa Issa!
“Issaaa!”
Dokta Katrina,akasema baada ya kumuona Issa hatoi mkono wake!Akakunja sura na kumkata jicho kali,ilielekea Issa hakuwa tayari kukubali yaishe.
“Issa haupo tayari?Niambie”
Katrina,akasema tena!Hapo ndipo,Issa akakubali kutoa mkono!Akasimama na kumkumbatia Deo kwa furaha!
“Maisha yaendelee Broo!”
Issa,akawa anampiga piga Deo mgongoni kwa furaha!Deo,akaanza kutabasamu nayeye akawa anampiga piga Issa mgongoni, akachukuwa kinywaji chake juu ya meza na kumuomba Issa wagongeshe glasi kuashiria amani itawale,wote wakasema ‘Cheeeeeers’ kwa furaha!Hiyo ikawa furaa kwa Dokta Katrina,akakwapua simu yake na kuanza kuwapiga picha.
“Tusimame jamani wote,tupige cheers”
Dokta Katrina,akashauri.Wote,wakanyanyua glass zao na kuzigongesha.
“Cheeeeeeers”
Kila mtu akasema!Kilichosikika ni glasi kugongana.Marietha,hakuwa na jinsi nayeye pia akaunga mkia.
“Hujambo wewe?”
Issa,akaanza kumchokoza Marietha!Siku hiyo walikuwa wenye furaha sana.
“Sema hujambo mke wangu”
Deo nayeye,akachomekea utani kidogo huku akicheka,kwa kweli ilikuwa shangwe!
“Ha! Haa! Haaa! Haaa! Haaaa! Haaaa! Haaaa!”
Issa akajichekesha.Katrina akawa amejawa na wivu kwa mbaliiiii!
“Mume wangu,njoo huku nawewe”
Katrina nayeye akamvuta Deo karibu huku akitabasamu!
“Sisi tushakuwa wahenga bwana.Na ndiyo wahenga tuliosema,anayekupenda mpende,asiyekupenda achana naye…Cheeeeeeerssssss”
Dokta,Katrina akatumia msamiati huo huku akiwa karibu na Deo wakagongesha glasi kwa mara nyingine na Deo,akawatizama Issa na Marietha.Sio siri,siku hiyo watu hawa walikuwa na furaha kupita kiasi.

********
Maisha ya Wiliam yalikuwa magumu katika ulimwengu wa mapenzi.Kutokana na mambo yaliyotokea, alisimamishwa chuo,kwake yeye kusimamishwa masomo halikuwa tatizo na hakuliwekea maanani.Jambo lililomuumiza ni kisura anayeitwa Karishma Issa Mpelembe!Huyu ndiye mrembo aliyekuwa anauzuzua moyo wake,akafa akaoza na ndiye sababu ya yeye kusimamishwa chuo!Bila ya Karishma maisha yake yalikuwa ni sawa na gari bila mafuta.Mbaya zaidi namba ya Karishma hakuwa nayo kwenye simu!Hata alivyoomba kwa marafiki zake,haikuwa rahisi kuipata.Wiliam, alisimamishwa chuo kwa muda wa Mwezi mmoja na nusu,ilimaanisha kwamba chuo kikifunguliwa ndipo adhabu yake itakuwa imekwisha,hakufikiria kuhusu adhabu aliyopewa!Kichwa chake chote kilijaa Karishma,hiyo ilifanya mpaka aachane na umalaya.Wanawake wote,aliokuwa anatembea nao,aliwaacha na hakuwa ana muda nao tena!
“Prisca,nimekwambia sikutaki usinifuate fuate.Mbona unakuwa hunielewi.Sitaki unipigie simu”
Siku hiyo Wiliam,alikuwa simuni anamtolea nje, mwanamke mrembo,ambaye alikuwa akitembea naye kimapenzi!
“Lakini Raphael,kwanini?”
“Kwanini?Sijui, lakini naomba tuachane kuanzia leo,usinijue jue.Fanya yako”
“Nakupenda Raphael”
“Kampende Mama yako mzazi”
“Rapahel tafa…”
“Prisca,achana namimi…tititi”
Wiliam,akakata simu na hivyohivyo aliwafanyia wanawake wengine wakina Diana,Malisa,Gradditute na Oddo!Alichotaka yeye ni namba za Karishma tu,wala sio mwanamke mwingine yoyote Yule.
Alitumia muda mrefu sana kumuwaza Karishma, kuliko adhabu yake ya masomo!Siku zake zilisogea kwa mwendo wa ajuza,hatimaye siku ya kufungua chuo ikawadia na siku hiyo, alihitajika kuripoti.
“Baba,ndiyo naenda chuo”
Siku hiyo William,alikuwa anamuaga Baba yake Mlezi huku akiwa ndani ya gari la kifahari aina ya Ramborgin,linalofunguka milango kwa juu,lilikuwa ni gari la gharama na zuri mno!Benton na Herrieth, walimpenda sana Wiliam ingawa hakuwa mtoto wao wa kumzaa!Ndiyo maana alidekezwa na kila alichokitaka alipewa.
“Usome Raphael”
“Nitasoma Baba”
“Nakupenda sana Raphael”
“Namimi nakupenda Baba”
Siku hiyo Herrieth hakuwepo,alikuwa nchini Marekani jimbo la Carlfonia kibiashara, ndiyo maana Wiliam alikuwa peke yake na Baba yake mlezi.
“Shika hii pesa!”
Benton,akamkabidhi Wiliam kiasi cha shilingi dola elfu mbili.Hiyo ikawa furaha sana kwake,akageuza gari na kuanza safari.Jumba lilikuwa kubwa sana kiasi kwamba kulikuwa kuna kama umbali wa mita mia moja mpaka kulifikia geti na alivyolikaribia tu,geti likafunguka, akalitoa gari nje na kuchukuwa barabara ya kuelekea Gulmashplan,kichwa chake kilijaa Karishma tu!Kitu cha kwanza baada ya kufika chuoni,aliingiza mabegi yake ndani ya chumba chake.Katika pita pita zake siku hiyo,akasikia mazungumzo ya chini ya kapeti ya kuwa Karishma anafika siku hiyo!
“Mmesema Karishma,anarudi leo?”
Wiliam,aliyaingilia maongezi ya wasichana wawili.Wakamuangalia kwa kitambo kidogo!
“Jamani,Karishma anakuja leo saa ngapi?”
Wiliam akauliza tena!
“Raphael,hata salamu?”
“Za saa hizi?Karshma anafika leo saa ngapi?”
“Saa kumi jioni”
“Na ndege gani?”
“KLM”
“Sawa”
Hizo zilikuwa habari njema kwa William,hapohapo akaingia chumbani kwake.Akajimwagia maji na kujipulizia marashi,akatafuta shati lake akapiga pasi vizuri.Suruali ya kadeti,akainyoosha pia!Akatafuta moka,nyeusi.Akaivaa.Siku hiyo alikuwa ‘smart’sana.Hakutofautishwa na mkurugenzi wa benki kuu ya dunia,na siku hiyo alikuwa tofauti kabisa na siku zote!
Kwani mara nyingi alikuwa akivaa kama wanamuziki akawa kama masharobaro.Siku hiyo hata yeye alivyojiangalia kwenye kioo, alikiri kwamba ametoka chicha.
“Hapa bomba,ngoja sasa nikampokee mtoto”
Wiliam siku hiyo alijisemea,akabeba funguo na kuingia ndani ya gari.Safari ya kuelekea uwanja wa kimataifa Arlanda ikaanza hapohapo,ndani ya lisaa limoja na nusu akawa anaingia uwanja wa ndege na zilikuwa zimebaki dakika kumi tu ili ndege ya shirika la KLM, iweke matairi yake juu ya nchi ya Sweden,jijini Stockhom!Ni kweli,baada ya dakika kumi kupita kipaza sauti kikasikika kwamba ndege hiyo tayari imetuwa.Macho ya Wiliam yalikuwa kodo,langoni’ terminal no 4’abiria walikuwa wakitoka na mabegi yao,wakiburuza!Dakika mbili zikawa nyingi,Karishma akatokeza.
“Karishmaa”
Wiliam,akatokeza kwa mbele yake mithili ya trafiki wa usalama barabarani anasimamisha gari.Ni kweli alikuwa ni Karishma na uzuri wake siku hiyo ulionekana kuzidi maradufu,hiyo ilimfanya Wiliam,apate kigugumizi cha ghafla.Cha ajabu hata Karishma,alionekana kupigwa na butwaa la waziwazi, baada ya kumuona Wiliam mbele,akiwa amependeza namna hiyo.
“Raphael”
Karishma nayeye,akaita huku akitabasamu!




Muonekano wa Wiliam mbele ya macho yake, ulikuwa ni wa utofauti kabisa,siku hiyo alivaa akawa kama mtu mzima mwenye heshima zake!Akamkagua kwa haraka kuanzia juu mpaka chini na siku hiyo ndiyo aligundua ya kuwa William ni mzuri na mtanashati,kuanzia nywele zake za usinga mpaka rangi yake ya mchanganyiko!Ndiyo maana akajikuta anapigwa na butwaa la waziwazi na kujikuta anaropoka bila kutarajia.Haukuwa utani,katika chuo kizima cha Stockholm alichokuwa anasoma Karishma hakuwahi kuona mwanamme mzuri kama Wiliam,lakini siku hiyo alimuona amekuwa zaidi ya Malaika.
“Pole na safari”
Wiliam,akamzindua Karishma kutoka katika bahari ya mawazo!
“Ahsante,ulijuaje nakuja leo?”
Karishma akauliza huku akiendelea kumkagua Wiliam,bado alishindwa kuelewa ni kwanini alikuwa akimtukana kijana mzuri namna hiyo,alitamani siku hiyo aombe msamaha.
“Niliota”
Wiliam,akatania.Karishma akatabasamu, hapo ndipo Wiliam alipohisi kwamba mbele yake amesimama malaika,sio siri Karishma alikuwa ni mrembo kwelikweli,sio uzuri tu peke yake, alikuwa anavutia na kwa mwanamme yoyote yule aliyekamilika ilikuwa ni lazima ageuze shingo yake nyuma,amuangalie na ndicho kilichokuwa kinaendelea ndani ya uwanja huo wa ndege,haikuwezekana hata kidogo mwanaume apite bila kumgeukia!
“Twende,nimeacha gari kule!Leta mizigo yako nikusaidie”
Siku hiyo Wiliam aligeuka nakuwa kama dereva wa taxi kwani alimsaidia Karishma mabegi yake,wakatoka nje ambapo huko kulikuwa kuna uwanja mkubwa wa kuegesha magari!Akatembea mpaka pembeni ya gari kali aina ya Ramborgin,akafungua kwa nyuma na kupakia mizigo.Akamfungulia Mlango Karishma!
“Ingia ndani ya gari twende”
Karishma,akaingia ndani ya gari.Hakuwa na jinsi,mbali na yote hakuelewa ni kwanini moyo wake siku hiyo,umeamua kutulia kwani ingekuwa kipindi cha nyuma asingekubali habadani kuingia ndani ya gari hilo,licha ya yote Wiliam angekuwa keshapewa majibu ya shombo!Vitu alivyokuwa anavifanya,alivishangaa mwenyewe!
“Sijakwambia,pole na safari.Vipi Afrika hawajambo?”
Wiliam,akavunja ukimya huku akihangaika kuligeuza gari!
“Hawajambo”
“Mama na Baba,wazima?”
“Wazima wote”
“Hawajani salimia?”
“Ha! Haa! Haaaa! Kwani wanakujua?”
“Ipo siku watanijua tu”
“Labda”
“Nikupeleke chuo moja kwa moja,ama tupite kidogo tukale?”
“Hapana,nipitishe chuo.Maana nimechoka sana.Nimekaa Amsterdam masaa mengi mno”
“Kwanini?”
“Kuna itlaf ilitokea kidogo”
“Pole sana”
Maongezi yao yaliendelea lakini ndani ya moyo wa Wiliam kulijawa shangwe ajabu.Hata yeye hakutegemea kama Karishma,angemchangamkia namna hiyo!Alivyotarajia na vitu alivyokutana navyo vilikuwa ni viwili tofauti,Karishma alikuwa ni msichana mwenye majibu machafu na hasira.Mbali na hapo Wiliam alishawahi kuogeshwa matusi na kisura huyu,licha ya yote hakukoma hata kidogo.
Alizidi kujipa moyo sababu aliamini ipo siku moja Karishma atakuja kuwa wake,hata kama ingemchukuwa miaka mia moja!Safari ilizidi kupamba moto,mpaka walivyofika chuo.
“Paki hapo tu”
“Hapana,nataka nikupeleke mpaka hostel kwenu”
“Tafadhali Raphael”
“Naomba ukubali”
Wiliam,hakutania alitembeza gari mpaka mabweni wanayoishi watoto wa kike, akapaki gari na kuteremka kwa mikogo,akamfungulia mlango Karishma ambaye siku hiyo alijihisi yeye kama Malkia vile na yupo peponi.Alivyoteremka kutoka garini,akasindikizwa mpaka chumba anachoishi huko alikutana na ‘roomate’ wake!Wakasalimiana na Wiliam akahaidi kuwa atarudi baadaye ili wazungumze!
“Ahsante Raphael”
“Usijali Karishma”
Wiliam,akatoka nje akiwa mwenye furaha sana siku hiyo.
Meno yake yote ameyakenua nje!Siku hiyo ikawa kama siku ya ushindi katika maisha yake,kabla ya kukubaliwa akaanza kutafakari siku ambayo ataona nguo ya ndani ya Karishma itakuwaje,akaanza kumvua nguo moja baada ya nyingine kihisia!Hicho ndicho alichokuwa anakiwaza kijana huyu mpenda ngono!Hata alivyofika chumbani kwake,alikuwa akimuwaza Karishma.
“Huyu Keshajaa kingi tayari,bado kumjaza kwenye kumi na nane!Ngoja nitumie gia ya kwenda taratibu kama kinyonga,nikienda pupa nitamkosa”
Wiliam siku hiyo alikuwa akitafakari mwenyewe, akiwa juu ya kochi,pembeni ana glasi ya pombe kali,kila kilichotokea siku hiyo kwake alikifananisha na ndoto ya mchana!Kuanzia siku hiyo Wiliam,akajifanya kuwa karibu sana na Karishma ilikuwa kila wakati wakitoka darasani ni lazima amtafute,wakae sehemu iliyotulia wapige stori za hapa na pale.Wiliam alitamani siku moja Karishma awe wake kimapenzi,waongee mambo ya mahaba lakini ilionekana vigumu sana sababu kila alipogusia maswala hayo Karishma alionekana kuchukia kupita kawaida,hakutaka kabisa kujihusisha na maswala hayo kwa wakati huo kwani ndani ya moyo wake,alimchukulia Wiliam kama Kaka!
“Tuwe Kaka na Dada tu”
Karishma siku hiyo,alifunguka!
“Kwanini lakini?Mimi naomba tuwe wapenzi”
“Raphael,haya maongezi sipendi yaendelee!Kuwa mwelewa”
“Mimi ni mwelewa.Lakini nawewe jitahidi kuwa mwelewa pia”
“Mimi msimamo wangu ndio huo”
“Kwani una mwanamme mwingine hapa Chuoni?”
“Hapana”
“Na yule jamaa,wa semista iliyopita.Jina lake limen’toka”
“Sina mahusiano naye”
“Kwanini usinipende mimi basi?Nakupenda Karishma”
“Hata mimi nakupenda,naomba tuwe hivihivi marafiki tu”
“Mimi nitashindwa”
“Kama ukishindwa,baasi”
Siku hiyo Karishma,alichomoa kwa mara nyingine!Haikuwa kwa Wiliam peke yake,hata mapedeshee wa kimarekani na ma Don,wenye pesa zao!Waligonga mwamba,Karishma hakuwa tayari kuwa na mahusiano ya kimapenzi,akiamini kwamba wanaume ni waongo,wanakuwa wana maneno matamu mno mwanzo lakini mwisho wa siku wakishaona vya ndani,wanakimbia!
Hivyo ndivyo alivyoamini kutokana na kusoma vitabu mbalimbali na kufuatilia filamu za mapenzi.Akakariri kuwa wanaume baba yao ni mmoja,hakuna yoyote mwenye nafuu,wote ni vichefuchefu.
“Siwezi kuwa nawewe Anthony,sitaki kabisa”
Siku hiyo akiwa kwenye mgahawa wa Mackdonald mjini,mzee mmoja wa kizungu alikuwa akimtongoza,akijaribu kumshawishi.Mzee huyu alikuwa ni mfanyabishara mkubwa!
“Kwanini sasa?Nataka nikuoe,uwe mke wangu mwingine unizalie watoto”
“Siwezi”
“Ukinikubali mimi nitakupa robo tatu ya utajiri wangu”
“Ahsante,nashukuru.Mimi sio Malaya”
“Sijamaanisha hivyo lakini”
Karishma,akachukia vibaya sana.Hakumalizia baga yake,akachukuwa simu yake na kutoka nje, ambapo huko alienda moja kwa noja kwenye stesheni ya treni za umeme,akaweka kadi yake vizuri ambayo ilitumika kama nauli.Alivyoingia ndani ya treni na baada ya abiria wote kupanda,treni ikachomoka kwa kasi ya upepo, mpaka alipofika,Hondol.
Huko akaenda kufanya manunuzi ya vyakula vya kupika kisha kurejea hostel.Jioni ya siku hiyo aliamua kwenda kukaa kwenye mgahawa mmoja, akiwa na kompyuta ya mapajani ameiweka mezani ili kuperuzi habari mbalimbali zinazoendelea!Alivyoridhika,akaiweka ndani ya begi na kuagiza kinywaji,hapo ndipo akapita Mwanamme mmoja,anayemsumbua kuliko kawaida!Mbali na hapo mwanaume huyo mzungu mweusi, alikuwa mvuta bangi na mkorofi.
“Leo nimekukuta kisura,Mambo”
Mwanaume huyo aliyefahamika kwa jina la Tonny Noris,alimsamilia Karishma kisha kuketi kwenye kiti cha pembeni.
“Poa,Tonny.Sitaki kuzungumza nawewe naomba uondoke”
“Niondoke vipi?Huwezi kuniambia niondoke”
“Basi baki mwenyewe”
Karishma alivyotaka kuondoka,Tony Noris akamshika mkono na kumkaliza kitini kinguvu!Akasogea karibu kabisa na kuanza kumshika shika kichwani.
“Tonny niache”
“Siwezi,leo mpaka nikunyonye denda”
“Tonny”
“Leta mdomo huo”
Tonny,akawa analazimisha.Kila kilichotokea kwa wakati huo wazungu waliona, lakini hawakutaka kuingilia wakijua watu hao wapo kwenye mahaba yao.
Tonny alikuwa ana mwili mkubwa, hivyo ilikuwa rahisi kwake,kumthibiti Karishma,akamvuta vizuri akijaribu kumsogeza mdomoni ili amnyonye mdomo,zoezi hilo lilionekana kuwa gumu sababu Karishma nayeye alijitahidi kukwepesha mdomo wake.Katika hali ya kushangaza, Tonny alihisi amevutwa kwa nguvu nyuma,akapigwa ngumi ya shavu, kuja kutahamaki vizuri alikuwa ni Wiliam!Haikujulikana alikuwa maeneo gani lakini kwa wakati huo,alionekana kuwa msaada mkubwa kwa Karishma!
“Achana na huyu demu, Tonny”
Wiliam akasema huku akiwa ametunisha kifua chake,alifanya hivyo ili kupiga mkwara, ukweli ni kwamba hata ingekuwaje asingeweza kushindana nguvu na jamaa huyo mweusi, aliyekuwa mwenye misuli mingi.
“Raphael,hiki ndicho nilikuwa nakisubiri kwa muda mrefu sana.Leo ndio Leo”
Tonny,akasimama wima na kumsogelea Wiliam,bila kuuliza chochote akamzaba kofi la uso,hakuishia hapo akamvuta na kumtandika kichwa cha pua.Wiliam, alivyotaka kurusha ngumi,ikadakwa akapigwa ngwala, akadondoka chini kama mzigo.Tonny,siku zote akitembea ilikuwa ni lazima awe na wahuni wenzake, watatu ama watano pembeni,hapo ndipo walisogea karibu na kuanza kumshambulia Wiliam kama mpira wa kona.
“Tonny,acheni.Toooonny”
Karishma alijaribu kuzuia ugomvi huo,Wiliam alikuwa akipigwa na kuchakazwa vibaya sana.Mbaya zaidi walikuwa wanampiga kwa zamu!Akitoka huyu,anaenda kwa yule.Wiliam akageuka na kuwa kama mpira wa danadana.Mwisho,akashikwa vizuri, akageuziwa Karishma!
“Huyu ndio bwana ako,si ndio?”
Tonny,akasema!Wakati huo Wiliam alikuwa akivuja damu mwili mzima,mdomo umeumuka vibaya sana!
“Tooonny tafadhali muachee”
“Subiri,tumfundishe adabu”
Wiliam,alipigwa tena.Kipondo kiliendelea bila kukoma,wazungu waliokuwa ndani ya mgahawa huo walikimbia na kuacha ugomvi unaendelea,mpaka walivyomuacha Wiliam,alikuwa anafanana na nyama buchani,anajiburuza kama jongoo!Maumivu aliyohisi mwilini,hayakuwa na mfano wake,alitambaa huku akiomba msaada!Kwa mbali alimuona Karishma akiwa na kundi la watu,wakamsogelea mpaka alipo.
“Huyu hapa,Raphael...Rapahel”
Karishma akaita kwa simanzi kubwa sana huku akiinama chini na kumtingisha,haikujulikana sura iko wapi miguu iko wapi.Hawakuwa na muda wa kupoteza,hapohapo wakafanya utaratibu wa kutafuta gari,wakampeleka hospitalini ili akapatiwe matibabu.

******
Wiliam alianza kupatiwa matibabu akiwa bado mwenye hasira,hiyo ni baada ya masaa matatu mengine kupita.Alivyokumbuka,kipondo alichochezea akatamani kusimama kutoka kitandani,aende kulipiza kisasi kwa Tonny,aliyemfanyia unyama huo!
“Raphael,punguza hasira”
Rafiki yake wa karibu,akajaribu kumtuliza.
“Hapana,siwezi kupigwa namna ile.Afe mimi afe yeye”
“Haipendezi,achana naye.Yule ni mvuta bangi unajua”
“Kama yeye anavuta bangi,mimi nakula”
Wiliam,siku zote alikuwa ni mtu wa visasi,hata siku moja hakukubali kupigwa na katika historia yake rekodi yake ilikuwa ndio hiyo.Kama akipigwa basi ilikuwa ni lazima amtafute mtu aliyempiga ahakikishe anampiga na kuchukuwa ushindi,hapo ndipo atakubali lakini kinyume na hapo,asingeweza kumuacha mtu huyo hivihivi.Hicho ndicho alichotaka kukifanya kwa Tonny,kulipa kisasi.
“Nataka niende hostel,anayolala Tonny,ameniumiza sana.Hawezi kunipiga mimi Raphael”
“Tafadhali”
“Nimesema hapana”
Alichofanya Wiliam ni kuchomoa bandeji usoni na kusimama kutoka kitandani,moyoni tayari alitengeneza bifu na Tonny,niya yake ilikuwa ni kutoka kitandani akapande Treni mpaka chuo ili aende hostel anayoishi Tonny, wakazichape usiku huohuo.
Lakini hakufika mbali,madaktari wakatokea na kumtuliza,ambapo walimchoma sindano ya usingizi,hiyo ndiyo ilikuwa njia pekee ya kumzuia.Lakini vinginevyo wasingeweza hata kidogo,kutuliza moto wake!

******
Hata hivyo hali ya Wiliam ilihimarika baada ya madaktari kufanya kazi yao vizuri,asubuhi ya siku iliyofuata, aliruhusiwa kutoka hospitalini ambapo alipokea pole nyingi kutoka kwa Karishma akimshukuru sana kwa kumuokoa kutoka katika mikono ya muhuni Tonny.Wiliam aliitikia na kujisikia furaha sana ndani ya moyo wake,namna ambavyo Karishma alionesha ukarimu wake ilimfanya ahisi kupona kwa haraka.Mbali na kujisikia vizuri lakini bado alikuwa ana hasira na Tonny Noris,hakutaka kukubali kupigwa ilikuwa ni lazima siku moja nayeye amtafute wapambane,huyu ndiye Wiliam,tabia yake ilikuwa ni hiyo, haikueleweka alirithi kwa nani.Siku mbili nzima, alikuwa akimuwinda Tonny,ajae ndani ya kumi na nane zake.Japokuwa alielewa vizuri ya kuwa Tonny ni bonge la jitu tena lenye misuli,lakini alijipa ushindi wa moja kwa moja na kuamini ni lazima amtembezee dozi nzito.
Siku moja akiwa kwenye mgahawa,akamuona Tonny akiwa na wapambe wake!Huo ndio ulikuwa muda muafaka wa yeye kuanzisha varangati,lakini hakutaka kukurupuka kwanza, alitaka kumbananisha Tonny akiwa mwenyewe,ndipo wapambane na wapimane ubavu.Wiliam hakuwa na nguvu lakini alikuwa ni mtata na mkorofi,ndiyo maana mbali na shule nzima kumjua kutokana na uzuri wake lakini upande wa pili alijulikana kutokana na utukutu wake.
“Huko huko naenda kumuanzishia.Naenda kupambana kufa kupona”
Wiliam,akaweka glasi ya juisi juu ya meza baada ya kumuona Tonny anaelekea upande wa chooni,nayeye akaunga kwa nyuma!Akazama chooni, ambapo baada ya kuingia alimuona Tonny anafungua mlango,yeye alivyozama ndani,akafunga mlango kwa ndani na ufunguo.
“Tonny”Akaita!
Kitendo cha Tony kugeuza shingo yake, bila kutegemea alipokea ngumi takatifu ya shingo,iliyokuwa kali sana.Wiliam hakuishia hapo,alimkamata mkono wake na kuuzungusha upande wa pili,ambapo alibamiza kichwa cha Tonny,juu ya kioo cha sink!Tonny akajua tayari hapo kuna kila dalili ya kupigwa kama asipojitetea,akajinasua na kumbeba Wiliam juujuu kama tenga la nyanya,hiyo ilikuwa rahisi kutokana na kuwa mwenye misuli,akamtupa Wiliam chini,akaanza kumshambulia na mateke!Wiliam nayeye hakutaka kukubali kupigwa,ndiyo maana akaudaka mguu wa Tonny na kuuvuta,Tonny akadondoka kama embe mtini, puu!Hapo ndipo Wiliam,akasimama kwa kasi na kumkaba kohoni kwa nguvu zake zote, mpaka Tonny alipohisi anaishiwa pumzi,ingawa alijitahidi kumtoa Wiliam lakini ilionekana kushindikana,Wiliam aliendelea kukaza mkono wake,hiyo ikafanya mpaka Tonny aanze kuishiwa nguvu,macho yakamtoka mithili ya mjusi aliyebanwa na mlango!
“Raph….ael nia…che uta..niu..aaaa”
Tonny alizungumza kwa shida tena kwa sauti ya mbali,koo lake lilikuwa limekabwa.Hewa haitoki na maumivu yalikuwa makali mno!Alijaribu kutapatapa na kumtupa William,lakini ikaonekana mambo yote yamegonga mwamba!Hiyo ilifanya mpaka ajambe ndani kwa ndani kwani pumzi ilishindwa kutoka puani!
“Omba msamahaaa,nakuuwa leo”
Wiliam,akasema kwa hasira huku akizidi kumkaba kwa nguvu!
“Raph..ael niachie”
“Nakuuwa”
“Nisa..me..heeee”
“Nisamehee nani?”
“Nisame..hee Rapha..el”
“Sema, Kaka Raphael kenge mweusi wewe”
“Ka..ka Ra..pha..el nisame..heeee.Nim..eko..sa”
Tonny,alikuwa amekabwa kisawasawa!Hakuwa mwenye ujanja na laiti kama Wiliam angeendelea kwa dakika nyingine sita,wenda angepoteza maisha, ndiyo maana akasalim amri!Wiliam akamuachia na kusimama kwa taadhari!Kutokana na roba kuwa kali,Tonny akashindwa kuinuka!
Kuanzia siku hiyo heshima ikawa imerudi,Tonny alimuheshimu Wiliam na kila akimkuta ilikuwa ni lazima ampe tano na kufurahi,wakageuka na kuwa marafiki wakubwa sana!

*****
Maisha ya Chuo,bado yaliendelea kuwa magumu kwake!Karishma alimnyanyasa kwa kiasi cha kutosha,mitego yote aliyotumia kumnasa ndege huyo mzuri ilifeli na kuonekana imegonga mwamba!Wiliam akahisi kuchoka,hakuelewa ni kwa namna gani nyingine afanye ili Karishma amkubalie wawe wapenzi!Mwezi mmoja mwingine ulikatika bila kuambulia chochote kile!Akahisi kukata tamaa lakini nafsi nyingine ilimwambia ipo siku Karishma atakuwa wake!
“Ngoja niendelee na mambo yangu.Sio rizki yangu!Nimemkumbuka sana Sesilia,nampigia simu sasa hivi na hili baridi,nataka aje kunipa joto muruua!Kichupa kimejaa”
William,alihisi kufanya ngono!Akili yake tayari ilikuwa imehama,akatamani kuwa na mwanamke kwa wakati huohuo afanye naye tendo baya la kuzini.
“Sesilia,uko wapi mahabuba wangu?”
Wiliam,alikuwa tayari simuni!Baada ya upande wa pili kupokea.
“Leo makubwa!Umenipigia?”
Mrembo huyo akaonekana kushtuka kwani Wiliam hakuwahi kumpigia simu hata siku moja.
“Nimekumisi,upo wapi?”
“Hondol”
“Panda treni uje”
“Wapi?”
“Njoo geto”
“Kuna nini Raphael?”
“Fuata nyuki ule asali,usiulize maswali”
“Una maana gani?”
“Nina maana uje kula asali”
Simu ilivyokatwa,Wiliam akaingia bafuni.Huko, alioga vizuri na kupiga mswaki ili kuweka mwili wake safi,tayari kwa mechi.
Kwa mwendo wa treni kutoka Hondol mpaka chuoni kwao,aliamini zisingezidi dakika kumi, ndiyo maana alifanya chapchap,baada ya kuoga akavaa taulo,ndani hakuwa na kitu chochote kile.Akavuta rimoti ya televisheni na kuiwasha.Ni kweli kitendo cha kuweka makalio yake juu ya kiti,mlango wake ukagongwa!Damu yake ikaanza kwenda kwa kasi,taulo lake kwa mbele likaanza kusimama, kuashiria kwamba nyoka wake,ana njaa ya kutema sumu.Alivyofungua mlango,akakumbana na mrembo huyu, Sesilia.Sijui kama alikumbuka kutoa salamu lakini hapohapo alimdaka na denda,akasukuma mlango huku akiendelea kumyonya mdomo!Mikono yake ikawa inapapasa,makalio ya Sesilia.Kutokana na moto aliokuwa nao,hapohapo akaanza kumtoa nguo zake kwa kasi,akamtupa juu ya kochi puu!Akatoa sidiria na kumvua nguo zote,nayeye akatupa taulo kando!Kazi yake ikawa ni kumtomasa kila sehemu ya mwili wake,akaipanua miguu yake huku na kule kisha kumuingiza nyoka wake ndani ya mgodi!Sesilia,akiwa chali,yupo katika sayari nyingine kabisa ya huba!Anatoa miguno,kwa mbali akaona mlango unafunguliwa,katika kumbukumbuku zake hakuwa mwenye uhakika kama walikumbuka kufunga mlango kwa ufunguo.
“Raph.aaaael aaashii aaaah aaaaah”
Sesilia,ndiye alikuwa anatoa sauti za puani na kwa wakati mmoja alikuwa akimuita Wiliam ili ageuke,aangalie mlangoni kwani kuna msichana aliingia akawa anawatizama.
Kwa upande wa Wiliam yeye ndio kwanza alikuwa ananyonga kiuno chake,anakazana. Hakuwa mwenye habari yoyote ile.Aliendelea kutoa dozi,akachukuwa miguu ya Sesilia,akaibana vizuri na kupeleka tena misumbwi.Sijui ni kitu gani,kilimwambia ageuke nyuma,moyo wake ukapiga paaa!Baada ya kumuona Karishma,amesimama mlangoni,anamwaga machozi!



“Unamsemea Raphael?Nani asiyejuwa kwamba hapa chuo kizima hakuna mwanamme kama yeye?Kwanza mzuri!Alafu anajua kuvaa,ananukia.Likitokea shindano la Mr.Stockholm University mwakani,lazima ashinde mimi nitampigia kura”
“Sema alivyoingia hapa chuoni,alikuwa anashobokewa!”
“Hiyo kawaida,mimi mwenyewe mpaka sasa hivi nampenda,ila sijui nitaanzia wapi.Anaringa sana”
“Lazima aringe,si mzuri”
“Inahusu?”
“Sema,nilisikia alishawahi kutembea na yule Madam wa Saikolojia”
“Acha utani,Yule Mbelgiji?”
“Huyohuyo”
“Wewe nani amekwambia?”
“Clara,alishawafuma mara kibao”
“Wapi?”
“Mara ya kwanza aliwafuma kwenye gari,mara ya pili aliwaona hotel ya Bulls,wapo pamoja!Alafu pia siku moja akawaona Bambataa, kwenye tamasha la Chriss Brown”
“Walimu wengine nao,kujipendekeza tuu!Yule si kama mtoto wake,amemzidi miaka”
“Umri ni namba tu siku hizi”
“Lakini hapa Ulaya,hawangalii hivyo vitu.Mwache ajilie vyake,hata mimi nampenda Raphael vilevile”
“Sasa hivi,amekufa ameoza.Kwa Karishma”
“Karishma huyu mgeni,Mwaka wa kwanza?”
“Huyo huyo”
“Anampenda sana Karishma,kaachana mpaka na mademu zake wote.Kisa Karishma”
“Hivi wewe,hizo habari huwa unatoa wapi?”
“Duniani,utanyimwa chakula lakini sio maneno”
Ndani ya darasa, siku hiyo baada ya kipindi kuisha,wasichana wawili walikuwa wakimjadili, Wiliam.Namna ambavyo alivyokuwa mzuri, mwenye mikogo!Hawa kuishia hapo,wote walimsifia kuanzia juu mpaka chini.Kilichomshtua Karishma aliyekuwa nyuma yao ni baada ya kusikia jina lake limehusishwa kwenye mazungumzo hayo,kwa mara ya kwanza alidhani wenda amesikia vibaya.Lakini alivyotega masikio yake vizuri,akajuwa kwamba ni yeye anazungumziwa,mbaya zaidi, katika majadiliano ya wanafunzi hao wakawa wanataja jina ‘Raphael’Mvulana aliyetokea kumsumbua kwa muda mrefu sana!
“Sasa hivi Raphael ametulia sio malaya kama zamani,anamfukuzia huyo Dada!Anaitwa Karishma,muafrika lakini rangi yake ya mchanganyiko”
Wakazidi kujadili,hawakuelewa nyuma yao Karishma yupo na anawasikiliza kila kitu wanachozungumza!
Kichwani kwa Karishma, ilikuja picha ya William,moyo wake ukaanza kuhisi kitu tofauti, hasa baada ya wasichana hao warembo walivyokuwa wanamsifia vilivyo,akajikuta anaona wivu ajabu lakini mpaka hapo!Hakuelewa kwanini hali hiyo inatokea,jinsi alivyohisi ilikuwa ni sawa na kipindi alivyokutana na Abraham,akaelewa kwamba anaanza kunasa taratibu ingawa hakutaka hali hiyo ijitokeze kwani hakutaka kujiingiza kwenye swala la Mapenzi hususani na Wiliam,alivyoona hali hiyo inataka kumzidi.
Akabeba ‘laptop’ yake na kuiweka ndani ya begi,hapo hapo akaelekea hostel, ambapo huko alijitupa kitandani na kuanza kutafakari juu ya maisha yake.
Sura ya Abraham pia ikamjia kichwani wakati huohuo,akakumbuka mara ya kwanza walivyokutana hotelini,wakazoeana kisha baadaye, akajitosa kimasomaso na kumueleza ya moyoni,yeye mwenyewe pia alikiri siku hiyo ya kwamba kila ndege hutua kwenye mti aupendao!Karishma akajifananisha na ndege na Abraham ni Mti.
Hata hivyo hakuelewa ni lini ama baada ya miaka mingapi,atakutana tena na Abraham,moyo wake ulitaka siku moja Abraham awe mpenzi wake na aliapia,huyo ndiye mwanaume ambaye atakuja kuiona nguo yake ya ndani kama angekutana naye siku moja.
Kitu kilichomuuma zaidi ni Abraham kutokupatikana simuni.Alitamani ajaribu tena namba za Abraham, lakini akakumbuka kuwa alizifuta namba hizo,akazidi kunyong’onyea!
“Nitakuwa na Raphael,kwa muda huu mfupi ili aniliwaze.Ngoja nimkubalie alafu nimuangalie kwa hizi siku mbili tatu”
Hivyo ndivyo Karishma aliamua kufanya,hakutaka kumkubalia Wiliam kutoka ndani ya moyo wake lakini ilibidi afanye hivyo ili walau amsahau Abraham,ndiyo maana dakika hiyohiyo akaingia bafuni kujimwagia maji,baada ya hapo akatoka na kanga mpaka chumbani!Akatafuta gauni lake jeupe la kubana,akalivaa!Gauni hilo siku zote, akilivaa ilikuwa ni lazima umbo lake nambari nane lijichore,akasogea mpaka kwenye kioo kikubwa na kukitizama!Alivyojiangalia kwenye kioo hata yeye alionekana kushtuka,figa yake ilimuogopesha!Karishma alikuwa ana mzigo nyuma na pembeni ana nyama zilizosambaa yaani ‘hips’!Akajikagua vizuri,akaona nyonga yake ilivyokuwa nyembamba na yenye mvuto.Siku hiyo hata yeye mwenyewe alijikubali ni mzuri,akaona ni sawa tu wanaume wanavyomsumbua na kugeuka kumuangalia.
“Naenda kwa Raphael,sasa sijui nimwambie nini?”
Karishma alizungumza mwenyewe huku akijizungusha zungusha,akiikagua figa yake.Alivyomaliza zoezi hilo,akabeba simu yake na kutoka nje!
Kitu kilichokuwa kichwani kwake ndicho kilichotokea,tangu akiwa anatoka mlangoni alijuwa ni lazima angegeuka na kuwa bango la matangazo,sababu watu wangemshangaa!Tangu Karishma aanze masomo chuoni hapo,hakuwahi kuvaa namna hiyo!Alizoeleka, akiwa ndani ya baibui na ushungi kichwani,siku hiyo kichwani hakuwa na kitu.
Nywele zake akawa ameziachia,hilo ndilo lilikuwa tatizo lingine pia!Hata wasichana wenzake walibaki kumshangaa.Kwa kuwa alitegemea kitu kama hicho,hakuona aibu tena.Akatembea mpaka block ‘C’ mabweni ya wavulana!Huko ndipo aliposababisha kasheshe lingine,wanaume walimmezea mate, wakamtamani kingono,umbo lake likafanya wengine wampigie miluzi.Haikufahamika alikuwa akijitingisha makusudi ili kuwatega ama ndiyo mwendo wake asilia, sababu namna alivyokuwa anatembea nyuma ilikuwa lawama,alikuwa akitingishika.Akatembea na kupandisha ngazi,chumba namba 16 ndipo alipokuwa anaishi Wiliam,peke yake!
Zilikuwa zimebaki mita kama nane ili aufikie mlango wa Wiliam,agonge kisha aingie.Kadri alivyozidi kupiga hatua kuufikia mlango,mapigo yake ya moyo yaliongezeka kudunda!Hakuelewa ni uwoga ama ni kitu gani,mbali na hapo hakujua ni jambo gani angemwambia Wiliam, endapo wangekutana macho kwa macho!Licha ya yote,hakutaka kuwaza sana sababu alijuwa kivyovyote vile, Wiliam angeanza kumtongoza upya,siku hiyo alipanga kumkubalia na waanze mahusiano rasmi!
Alivyofika mlangoni,akagonga mara mbili.Ukimya ukamfanya ajaribu kama mlango upo wazi,akanyonga kitasa!Lakini sauti zilizokuwa zinatoka ndani zilimfanya asite kidogo kwa kudhani wenda Wiliam anatizama filamu chafu za kikubwa, kumbe haikuwa hivyo.
Hakuamini macho yake,baada ya kuzama ndani.Wiliam alikuwa yupo juu ya kiuno,uchi wa mnyama.Makalio yapo wazi,anazungusha kiuno chake,anafanya tendo lililomleta duniani!Hapo ndipo akahisi kama nguvu za miguu zimemuishia,alitamani kugeuza lakini alishindwa kwani butwaa alilopigwa halikuwa na mfano wake.

Mbaya zaidi katika maisha yake,hakuwahi kuona binadamu wakifanya mapenzi ndiyo maana hiyo ikachanganya, kuduwaa kwake.Kwa kama sekunde nane,ndipo William akageuka, wakaonana macho kwa macho,akawa kama amezinduka sasa kutoka usingizini.Kwa kasi ya roketi akatoka nje huku akitembea hatua mbilimbili!Kila mtu aliyekutana naye,alimshangaa!
“Raphaaael”
Mrembo aliyekuwa na Wiliam,aliita baada ya kumuona Wiliam, amesitisha mchezo huo ambao kwake ulianza kunoga!
“Niache kwanza”
Wiliam,akasema.Nayeye alionekana kuchanganyikiwa kuliko kawaida,akavuta boxa yake iliyokuwa chini na kuiweka mkononi kwa niya ya kuivaa lakini akashikwa mkono na Sesilia!
“Raphael,njoo tumalizie”
Sesilia,akaongea kwa unyoge na macho yake yalikuwa yamelegea,juu ya kochi anamuangalia Wiliam,akamshika mkono ili warudi kwenye mchezo huo,wamalize biashara!
“Sesi,niache”
Wiliam,akachukuwa kaptula akaivaa,akavuta shati na kuliweka mwilini bila ya kufunga vifungo,akachomoka kama mkuki.Alivyotokeza kwenye korido akamuona Karishma, ndiyo anaishia kutoka nje ya hostel,akaanza kushuka ngazi mbilimbili huku akiwapiga watu vikumbo,ilikuwa ni lazima amuwahi Karishma amuelezee ingawa hakujua ni kitu gani amwambie.
“Karishmaaa,Karishmaaa”
William,alianza kuita huku anamkimbilia msichana huyo mrembo aliyetokea kuuteka moyo wake mazima!
“Karishma”
Alivyomfika akamshika bega!
“Karishma,nisikilize”
“Niachee Malayaaa”
Karishma akajibu,macho yake yalikuwa mekundu kwa ajili ya kulia.Hakutaka tena kumsikia mtu anayeitwa Wiliam katika maisha yake,moyo wake ulimuuma ajabu.
“Karishma nisikilize”
“Nikusikilize nini?”
Karishma akajibu na kuutupa mkono wa Wiliam pembeni,akachapa mwendo!Hatua alizokuwa anapiga zilitisha,kwa mwendo wa haraka bila kuangalia nyuma, akafika ndani kwake na kujitupa kitandani,Wiliam nayeye akazama mpaka ndani bila kuambiwa karibu.
“Karishma nisikilize”
“Niache nimekwambia,nani amekwambia uingie ndani kwangu tookaaa Raphael.Nenda kwa mwanamke wako.Bora hata Mungu amenionesha mapema ushenzi wako”
“Sio hivyo Karishma,nisikilize”
“Sina cha kukusikiliza,tokaa”
Karishma alizungumza kwa uchungu sana,machozi yakiwa yanamtiririka.Akachukuwa kitambaa na kujifunika usoni!Akawa analia ndani kwa ndani,kohoni kwake alihisi kama kuna gubu limemkaba na ili litoke, ilikuwa ni lazima atoe machozi!
“Karishma nisikilize”
Wiliam,akamsogelea Karishma karibu kabisa,akamshika bega!
“Haina haja,kwa..ni..ni nikusikilize kwani mimi si dada ya..ko?Nime..furahi kumjua wifi yangu”
Karishma alikuwa akizungumza kwa kwikwi,hakutaka kuonekana analia machozi kwa ajili ya Wiliam,kwa kufanya hivyo alijuwa ni lazima Wiliam angechukulia huo ndiyo ushindi na udhaifu.Hakuelewa kwamba, amechelewa kwani kulia kwake Wiliam alichukulia kama kuchukuwa ubingwa,Wiliam hakuwa mgeni katika swala la mapenzi,siku hiyo alishangaa na kwa asilimia mia moja, aliamini ni lazima Karishma analia kwa ajili yake,akajijibu kwamba, mrembo huyo ni wake kwahiyo ilibidi ajiongeze!
“Karishma,futa machozi.Usilie,naomba nikueleze ukweli”
“Sitaki kujua”
Alichofanya Wiliam,akamsogelea karibu kabisa na kumshika nywele!
“Una nywele nzuri sana.Laini laini”
Wiliam,akajaribu kubadili mada ili acheze na saikolojia ya Karishma, akachomekea vibonzo kidogo na kuingiza mada nyingine,ilikuwa ni wazi kabisa kama angeendelea kuomba msamahaa isingewezekana kwa Karishma kukubali kizembe kwani aliamini ni mwanamke mwenye misimamo mikali, mbali na hapo hata angemuimbisha kuhusu maswala ya mapenzi ingekuwa vigumu kwa mrembo huyu,kulainika!
“Una macho mazuri pia.Ukinuna wala hupendezi”
Wiliam,akawa kama mtu anayezungumza na sanamu sababu Karishma, hakujibu kitu chochote kile alibaki ameganda,amevimba kama chura!Wiliam akazidi kupapasa nywele zake, zilizokuwa laini kama sufi,kuna hali ambayo Karishma alianza kuihisi isiyokuwa ya kawaida.
Mkono wa Wiliam ulivyopita shingoni kwake,akahisi kama amepigwa na shoti ya umeme,akatulia kidogo.Wiliam akaendelea kuchezea nywele za mrembo huyo,ambaye alikuwa ametulia kama kitoto cha paka, akapitisha mkono shingoni kwake akawa kama anamkwaruza na kucha,akapandisha mkono wake juu kidogo na kuanza kumpapasa Masikio,hapo ndipo Karishma akahisi mwili wake wote umekufa ganzi,katika maisha yake tangu azaliwe hakuwahi kukumbana na hali kama hiyo.Wiliam akazidi kumsogelea karibu Karishma,akasogea tena karibu zaidi,akazungusha mikono yake mabegani mwa Karishma,akasogeza mdomo karibu!Katika hali ya ajabu naya kushangaza Karishma hakupindisha mdomo wake,akawa ametulia mpaka ‘lips’ zao zilipogusana,Wiliam akatumbukiza ulimi ndani ya kinywa cha Karishma,moyo wa Wiliam ukakita kwa nguvu.Karishma akaachanisha meno yake,ulimi wa Wiliam ukapita mpaka ndani.Hakuwahi kupigana denda,hiyo ndiyo ilikuwa mara yake ya kwanza kubadilishana mate tangu azaliwe,ndiyo maana akahisi kutetemeka ajabu.Alitamani, kumsukumiza Wiliam atoke lakini ilishindikana kwani alihisi yupo dunia nyingine tofauti,akafumba macho yake akawa anasikilizia vitu fulanifulani ambavyo hakujuwa vimetokea wapi!Hata angepewa kalam na karatasi angeshindwa kabisa kuvielezea.Wiliam hakuishia hapo,tayari kwake yeye kufanikisha kumla denda Karishma ulikuwa ni ushindi tosha,akachomoka mdomoni mwa Karishma na kuanza kumnyonya shingo.
“Mmmmmmmh”
Karishma akatoa mguno wa ndani kwa ndani,hapo alikuwa hajiwezi tena!Akawa amelewa kabisa,mtoto huyu fundi hakuishia hapo!Mikono yake,akaipitisha kifuani mwa Karishma akawa anachezea maembe yaliyokuwa laini kabisa,akawa kama anayabinya kwa mbali huku akiendelea na zoezi la kumyonya shingo, Karishma.Siku zote,mchofya kibuyu cha asali huwa hatosheki ni lazima tu atataka aendelee,hilo ndilo lililotokea kwa Wiliam.Mkono wake akauweka mapajani mwa Karshma,akaivuta sketi yake kwa juu,akauingiza ndani kabisa.Akazidi kuupandisha juu,lakini alivyofika karibu na mgodi, mkono wake ukazuiwa.Hapo Karishma akawa kama ameshtuka kutoka usingizini,akamsukumiza Wiliam kwa nguvu, kando!
“Raphael,toka tafadhali”
“Kar…”
“Hapana ondoka”
Karishma,akaropoka kwa sauti na kuweka nguo yake sawa!Akasimama wima na kuanza kumfukuza Wiliam aondoke nje,alihisi kujuta kwa kitendo alichokuwa anakifanya.Pepo la ngono likawa limemtoka!
“Raphael ondoka”
Wiliam,hakuwa na sababu ya kuendelea kubaki tena ndani ya chumba hiko.Akaondoka zake huku moyoni akiwa amejiwekea ushindi wa mia kwa mia wa kumpata kisura huyo!
Wiliam,hakukoma aliendelea kumlia mingo Karishma kila kukicha,akawa anamtumia meseji za mapenzi kwenye simu yake, akimuomba awe wake!Hakutaka kukata tamaa kirahisi,alitamani siku moja awe mpenzi wake.Aliapia siku ambayo Karishma atamkubali,atafanya sherehe ndogo ya kuwaalika watu wanywe na wale.
Na kweli,hazikupita hata wiki mbili,Karishma akajikuta amenasa kimapenzi kwa Wiliam.Siku hiyo chuo kizima kilijuwa kwani ilitokea sherehe,Wiliam aligharamia.
Akavimba,wanafunzi wengi hususani waliotoswa na Karishma walilitafsiri jambo kama hilo ni ndumba,wakaamini wenda Wiliam anatumia kizizi.Haikuwezekana hata kidogo mrembo kama huyo, kukataa zawadi za magari na fedha,akamkubali Wiliam tena kicheche,Malaya mbwa!Habari za Wiliam kuwa Malaya, Karishma alizisikia sana na wanafunzi wenzake walimshauri na kumwambia,ameingia choo cha kike yaani atakuja kujuta, katika maisha yake yote!
“Nijute,nisijute.Ni maisha yangu,nimechoka na hizo habari zenu kila siku.Hamna vitu vingine vya kufanya?”
“Utakuja kujuta”
“Kwanini?”
“Ni Malaya huyo Raphael”
“Ndicho nilichompendea”
Hayo ndiyo yalikuwa majibu ya Karishma kila kukicha, akaweka masikio pamba akageuka na kuwa sikio la kufa.Mwishowe walichoka kumgasi na kumpa habari za Wiliam!

*******
“Hapana,siwezi kuja kulala kwako Mpenzi.Siku nyingine”
“Lini sasa?”
“Nitakwambia”
“Nakupenda Mpenzi”
“Mimi pia”
Siku hiyo Wiliam na Karishma walikuwa wakiagana,siku zote Waliishia kupigana madenda.Kila Wiliam, alipojaribu kuomba penzi,Karishma alimpiga chenga akimpa sababu nyingi,siku hiyo ikapita.Wiliam,akawa msumbufu. Alitaka siku moja afanye ngono na mpenzi wake lakini aliishia, kupigwa kalenda kila kukicha.
“Ndo leo sasa!”
“Sikukwambia juzi”
“Kitu gani?”
“Leo nipo kwenye siku zangu”
“Kweeeli?”
“Ndio”
Karishma siku hiyo akawa ametoa sababu nyingine akamchenga,ukweli ni kwamba hakuwa tayari kuruhusu Wiliam aone nguo yake ya ndani,isitoshe alikuwa bado bikira!Vitu hivyo viwili vilimfanya aogope sana kumueleza William,alikuwa ni mwenye wasiwasi mkubwa wa kuchukuliwa yeye ni mshamba kwani katika fikra zake aliamini kuwa wanawake wenye bikira wanachukuliwa ni washamba, hawajui kitu,hakuwa tayari kumwambia ukweli William.
Siku zilizidi kwenda na habari ilikuwa hiyohiyo,kila kukicha Karishma aliibuka na sababu.Mara kichwa,mara Maralia,Mara homa!Hiyo ilimkera sana Wiliam lakini alivumilia akiamini Karishma ni ndege wake na hakuwa na sababu ya kutumia manati.Mwezi ukakatika bila ya Wiliam kugusa tunda la Karishma,siku hiyo Wiliam akaamua kufunguka, baada ya mambo kumfika shingoni.
“Hivi?Una bwana mwingine au?”
Wiliam siku hiyo aliuliza baada ya kumla denda usiku,wakawa wanaagana kulala.
“Kwanini?”
“Maana sielewi,haya ni mapenzi gani?Yaani mimi naishia kunawa tu.Kula sili,ndiyo nini sasa?”
“Una maana gani Raphael?”
“Wewe hujui, au?”
“Ndio”
“Mimi niishie kukubusu tuuuuuu.Nini maana ya kuwa wapenzi?Mimi ni kaka yako kwani?”
“Kila kitu kinahitaji utaratibu mpenzi”
“Utaratibu gani?Mimi nimechoka,nimevumilia kwa mwezi mzima.Mimi ni binadamu ujue”
“Kuwa na subira”
“Hapana,mimi nitashindwa”
“Utakuwa hunipendi,mapenzi sio ngono”
“Kumbe ni nini?”
“Usiku mwema Mpenzi”
Karishmna hakutaka kuendeleza hoja hiyo,akataka kuondoka William akamshika mkono!
“Hatujamaliza kuongea”
“Tutaongea kesho”
“Kesho usiponipa,mimi nawewe basiii”
Wiliam,akawa anatingisha kiberiti akitaka kujua kama kina njiti.Ukweli ni kwamba njiti zilikuwepo lakini zilikuwa zimelowa,zisingewaka! Kumaanisha Karishma hakujibu kitu chochote wala kushtuka, akaondoka zake huku nyuma akimuacha Wiliam anamsindikiza kwa macho,mbaya zaidi Karishma alikuwa amevaa suruali,hiyo ikafanya atingishike kwa nyuma,William akazidi kupata miyemko akatamani siku hiyohiyo awe na Karishma kitandani,akidhi haja zake!
Ilikuwa ni wazi ya kwamba, tangu Wiliam aingie katika ulimwengu wa mapenzi,hakuwahi kuburuzwa na kuendeshwa na mwanamke yoyote Yule isipokuwa Karishma,alikuwa ana penzi la kijeshi!Wiliam aliburuzwaburuzwa kama gari bovu,kama Karishma akisema ‘NO’ ujuwe ndiyo,hivyohivyo.
“Yaani huyu mtoto ananifanyia hivi,kisa sijamtia.Nikimvua nguo yake ya ndani atanikoma naona heshima itakuwepo”
Hivyo ndivyo Wiliam,alivyoamini ya kwamba kiburi cha Karishma kilichangiwa kwa sababu hakuwahi kulala naye kitandani yaani hakuwahi kuona nguo yake ya ndani,ndiyo maana akawa ana jeuri.
“Eti leo,hajisikii kuonana na mimi,Kweeeli?Sijui kwanini nimemuonesha nampenda hivi,acha niwe fala tu”
Siku hiyo Wiliam,alijiongelesha mwenyewe baada ya kutoswa kuonana na Karishma!
Siku moja maji yalimzidi,akanywa pombe nyingi ili akamtolee povu, Karishma!Badaa ya kuwa bwii, usiku wa saa mbili,akaibuka hostel ya Karishma ambapo huko alimkuta yupo na marafiki zake,wanasoma!
“Hayaaaa,nyieee Muda wa kulala huuu.Hamna wanaume nyieee?”
Wiliam,akaongea na sauti yake ilionesha kwamba yupo mtungi!
“Nasema hiviii,ninyiii hamna wanaume wa kuwakuna,hivyo vidude vyenu.Hamna mabwana,ayaa poteeni.Upesiiiii”
Kwa kweli aliogopeka,kila mgeni siku hiyo alitafuta kona yake!Karishma akabaki peke yake,amevimba kwa hasira kama chura!
“Ndio nini sasa?Wala sijapenda”
“Hujaaapendaaaa niniiii?Huna lolote,mnafki tuuu”
“Mimi?”
“Kwani hapaaaa tupooo wangapiiiiii?”
Wiliam,alivyozungumza hivyo akawa anageukageuka kwa vitendo ili kupigilia msumari sentensi yake.
“Nakuuuliza,kwaani hapa tupo wangapi?Ninaongeea naweweee”
“Unataka nini sasa hivi?”
“Nataka kuzungumza nawewe,hivii utanibania mpakaaa liniiiii?Siwezi kula ugali kwa picha ya Samaki,hata kidogooo.Upoo?”
“Tueshimiane Raphael”
“Hakuna cha heshima hapa,nataka tuwekane waziiiiii, kabisaaaaa!Au mpaka unataka sikuu usikie Raphael kabaka mbuziii,ndiyo uanze kujuta”
“Kaa chini nikwambie ukweli”
Wiliam,akamwangalia Karishma kwa kama sekunde kumi!Kisha,akakaa!
“Aya,nipangeeeee”
“Mimi ni Bikira”

******
Abraham akawa amerudi katika hali yake ya kawaida.Lakini hakuwa mwenye amani sababu hakupata mawasiliano tena na Mama Maria,mkataba wao wa mapenzi ukawa umekwisha!Kuanzia siku hiyo mawasiliano yakakatika sababu tu Abraham alibadili namba pia,hata hivyo bado wanawake waliendelea kumgasi,haikuwa rahisi kumpata lakini bahati hiyo ikamdondokea msichana mmoja mrembo kuliko kawaida!Hiyo ni kutokana na msichana huyo kutokata tamaa.Kumtomgoza Abraham ilikuwa yataka moyo, na ilikuwa ni sawa na kutuma maombi ya kazi Ikulu,Abraham hakuwa mrahisi kama wanawake wengi walivyodhani.
Kila kitu kikaonekana kuwa furaha kwa Janeth Riwa!Alikuwa ni binti mrembo Mfupi kiasi,nyuma amebinuka kimtindo,rangi yake ilikuwa nzuri ya chocolate!Hapo ndipo Abraham alipokuwa ameamua kutulia!Alimuonesha mapenzi yote.
“Love,nakupenda sana!Naomba usije ukaniacha,naelewa wanawake wengi wanakupenda”
Siku hiyo,Janeth Riwa alimwambia Abraham!Penzi lao lilikuwa bado bichi tena motomoto,hivyo alikuwa anajihami!Penzi la Abraham na Janeth lilipamba moto,kila usiku ilikuwa ni lazima wazungumze mambo mbalimbali, hususani michakato na malengo yao kwa ujumla!
“Hivi,Abraham”
Ulikuwa ni usiku wa saa tano siku hiyo,Abraham yupo kitandani ameshakula, anazungumza na mpenzi wake!
“Naam”
“Utakuja kunioa?”
“Ukiwa muaminifu,ndiyo utakuwa mke wangu”
“Abraham,nakupenda sana!”
“Mimi pia”
“Umevaa nini?”
“Boxa na vest”
“Nije?”
“Njoo…”
“Nakuja mpenzi…Hivi,ukishikwa wapi huwa unapagawa?”
Janeth,akaanza kumchimba Abraham.Alitaka kujua sehemu zake dhaifu!Alikuwa ana haki ya kuuliza sababu alitaka kujuwa.
“Kifua”
“Kifua tu?”
“Baby,utajua ikifika siku”
“Lini?”
“Jumamosi”
“Wapi?”
“Utakuja home”
“Kweli Love?”
“Ndio baby”
“Ninataka uenjoy,nakuhaidi nitajitahidi ufurahi”
“Mimi yangu macho tu”
Abraham na Janeth,wakawa tayari wamepanga wakutane chumbani wafaidi tunda.Ilielekea siku zote, siku ya Jumamosi Deo Karekezi na Marietha hawashindi nyumbani,hivyo nyumba wanamuachia Abraham peke yake!Huo ndio mwanya aliotaka kuutumia Abraham,siku ya Jumamosi.

Ilikuwa ni siku ya Jumanne,kuanzia siku hiyo.Sio Abraham wala Janeth, kila mtu aliona siku ya Jumamosi ni kama Mwaka vile.Siku zilijisogeza taratibu na mwisho wa siku,Jumamosi,ikawadia!Abraham siku hiyo alivyodamka asubuhi,alifagia chumba chake,akapiga deki mara mbilimbili.Akapanga kila kitu sawa kwani siku hiyo alikuwa ana ugeni mkubwa,kwa mara ya kwanza, alikuwa akienda kumvua nguo ya ndani Janeth,akaanza kupiga picha jinsi, itakavyokuwa!Akatamani,asukume muda mbele uende harakaharaka!
“Shikamoo Baba,Shikamoo Mama”
Alivyotokeza mlangoni,akawasalimia wazazi wake ambao tayari walikuwa wamejiandaa kwa safari ya kuondoka!
“Marahaba”Marietha na Deo,wakaitikia kwa pamoja!
“Abraham”
“Naam Baba”
“Sisi tunatoka,tunaenda shamba Korogwe!Usisahau kufunga milango!Nitakutumia pesa nyingine ya kula Tigo pesa,kwenye friji kuna chakula nadhani”
Baba akawa anatoa maelekezo.
“Shika hii elfu kumi,weka mfukoni”
Baada ya maelekezo hayo,wazazi wake wakaondoka!Hatimaye, Abraham akawa amebaki mwenyewe ndani ya nyumba,akashuhudia mpaka gari linavyotoka nje na geti kujifunga!Akaingia ndani,chumbani kwa wazazi wake na kuchukua marashi ya kunukia,akaenda kupuliza chumbani kwake!
Chumba chake kikawa kinatoa harufu nzuri.Akaingia bafuni,akajimwagia maji,akavaa na kwenda mezani kunywa chai.Alivyoingia chumbani akakuta ‘Missed call’ nane kutoka kwa Janeth,alivyoingia kwenye uwanja wa meseji, akakumbana na meseji ndefu,moyo wake ukapiga paaa!Kwani kwake ujumbe huo
ulikuwa wa kutisha!

*******
Siku zote tabia ni kama ngozi,kamwe huwezi kuzibadili!Mbali na Wiliam kuwa na Karishma kimapenzi,alirudi na kuendelea na tabia yake hiyohiyo!Ki ukweli hakuweza kuvumilia mpaka ndoa, ndipo apewe penzi,sawa aliitikia ya kuwa atavumilia kwa kuwa Karishma alidai kuwa ni bikra!
“Bikra Bikra bikra,Bikra gani?Mademu wengine ni wasaniii,eti mpaka ndoa!”
Siku hiyo Wiliam,alijiongelesha mwenyewe akiwa chumbani kwa rafiki yake,aliyeitwa Carlos Santana!Humo ndimo aliamua kukutana na msichana mwingine anayeitwa Nadia,aliogopa kutumia chumba chake,kumuhofia Karishma wenda angemkuta na akaunguza picha!Ndiyo maana, akampanga rafiki yake siku hiyo,amuachie funguo ili amshughulikie,kisura huyo Nadia.Hicho ndicho kilichotokea,Kwa kuwa Nadia alijua ni kitu gani,kinatakiwa kufanyika.Alivyozama chumbani tu, mwenyewe akaanza kurembua!Wiliam,hakuremba!Akamvuta mdomoni na kuanza kumla denda,mkono wake ukapita chini ya sketi fupi, ukakumbana na mgodi wa mrembo huyo,hapohapo akaanza kupima oil, ili ajue kama ni bwawa au kisima!


Hapakuwa na wakati wa kupoteza,kwa muda wa karibia sekunde tisa nzima walikuwa wakipasha.Kila kitu kilivyokwenda sawa, Wiliaam akaanza makamuzi!Siku hiyo Nadia alilia na kutoa sauti za puani kama kitu gani sijui,haikufahamika kama ni utamu kolea ama anapata maumivu!Wiliam siku hiyo ilikuwa ni kama amemeza vidonge hatari vinavyoitwa Viagra,vya kufanya udumu ndani ya ulingo kwa muda mrefu!Kwani alimkamua Nadia kuliko kawaida,kazi yake ilikuwa ni kumgeuza geuza kama mtu anayechagua embe gengeni.Ilikuwa mara amuweke mbuzi kagoma kwenda majanini,mara kifo cha mende.Na mikao mingine haikufahamika vizuri kwani wakati mwingine Nadia alikuwa anakunjwa kunjwa,Wiliam alikuwa ni mtundu kitandani,ndiyo maana alivyopachika mpira nyavuni,akaunganisha bila refa kujua!Mpira ukawekwa kati,mechi ikaendelea!Ingawa jasho kwa mbali lilikuwa linamtoka lakini haikumfanya asitishe mechi hiyo ya kukata na shoka!Kwa Nadia tangu,amfahamu Wiliam,hakuwahi kufanyiwa vitu vya nanma hiyo hilo alikiri kimoyomoyo!Wakati mwingine mpaka kiuno kilikuwa kinamuuma.Lakini alijikaza kisabuni sababu hakutaka kuonekana mzembe,japokuwa alijitahidi nayeye kutaka kuonesha maujuzi lakini ilishindikana,Wiliam alionekana kuumiliki mpira kwa kipindi cha muda mrefu,ndiyo maana Nadia akawa amefichwa!Mambo yaliendelea,mpaka Wiliam anapachika mpira nyavuni akishinda magoli matatu yeye Nadia alikua hoi kwa magoli saba,hiyo kwake katika ulimwengu wa mapenzi akawa amevunja rekodi,haikuwahi kutokea hata siku moja!Wiliam alikuwa ametulia juu ya kifua chake,anahema ndani kwa ndani!Anajihisi mwepesi kama mfuko wa pamba!
“Pole sana mpenzi”
Nadia akazungumza kwa sauti ya mahaba,akiwa chini.Wiliam bado yupo juu yake,wapo uchi wa mnyama!
“Ahsante”
“Nani alikufundisha haya mambo Raphael?”
“Mambo gani?”
“Mmmh,kwani hujui?”
“Sijui ndio”
Wiliam,akajifanya hajui lolote.Niya yake alitaka tu, asifiwe!
“Mambo uliyotoka kunifanyia”
“Hayo kawaida tu”
“Lakini Raphael,kwanini unapenda kuniumiza?”
“Kivipi?”
“Una wanawake wengi”
“Sasa naona umeanza!Kwanza naomba niondoke,nina ratiba fulani hivi baada ya dakika thelathini”
“Basi samahani mpenzi”
Nadia akadhani labda maneno aliyozungumza yalimkera Wiliam,ndiyo maana akawa mpole kama njiwa aliyemwagiwa maji!
“Baadaye basi,alafu usinipigie simu.Mimi ndiyo nitakutafuta”
“Lakini Ra…”
“Kuwa mwelewa basi”
Wiliam,akatumia utemi.Na alizungumza akimaanisha sababu alianza kusimama na kuokota nguo zake zilizokuwa chini.
“Sasa uogi?”
Nadia akauliza kwa niya ya kujikomba,alishaelewa tayari yakuwa William amekasirika hivyo ilibidi ajirudi sababu alikuwa akimpenda bado!
“Nitaoga kwangu”
“Ayaaa”
Nadia aliitikia kinyonge,moyoni aliumia lakini hakuwa na jinsi zaidi ya kukubali matokeo!Alibaki juu ya kitanda,anamshuhudia Wiliam anamaliza kufunga vifungo vya shati,akamuona anafungua mlango na kuondoka zake!

Karishma hakumsumbua kichwa chake tena!Alishapata suluisho la tiba yake,Wiliam aliendelea na tabia yake ya kishenzi,kuchepuka na kuwa fisadi wa mapenzi.Akaendelea kuwagonga wanawake kama kawaida, akazidi kuwachanganya kama pilau na kachumbari,wakati mwingine hakuremba!Alilala mpaka na vibibi vizee.Kifupi mtoto huyu haikujulikana kama alikuwa ana pepo la ngono ama amerithi.Mchezo huo kwake ulikuwa mtamu kiasi kwamba hakuweza kupitisha siku bila kumvua mtoto wa kike nguo yake ya ndani ili amsosomole, asipofanya hivyo ilikuwa ni lazima aweweseke usiku kama teja aliyekosa kujidunga sindano ya unga,ama kifupi angepatwa na arosto!Mbali na hapo tabia hiyo aliifanya kwa siri kubwa sana!Wengi wao walidhani wenda Wiliam amebadilika kwani hakuwaingiza wanawake ndani ya chumba chake bali hotelini na nyumba za wageni.
Wakati mwingine alidiriki kufanya ngono hata chooni,hakuogopa pia kudinya ndani ya gari.
Kufikia hapo,hakumsumbua tena Karishma kumuomba penzi,hilo lilimfanya Karishma ajipe asilimia mia kwa mia yakuwa Wiliam,amebadilika na ana mpenda kweli.
“Nakupenda Karishma,ndiyo maana nimeamua kutulia.Nasubiri mpaka siku tufunge ndoa, kama unavyotaka”
Hayo yalikuwa maneno ya Wiliam siku hiyo wakiwa ndani ya mgahawa wa Mackdonald,uliopo maeneo ya T- centrialaren na alikuwa akimueleza Karishma kwa hisia zote!
“Hata mimi nakupenda Raphael,bikira yangu ndio itakuwa zawadi yako”
Karishma alikuwa ana kila sababu ya kuyaamini maneno ya Wiliam kwani ilipita zaidi ya miezi miwili tangu Wiliam aache kumsumbua kuhusu kufanya mapenzi, mbali na hapo habari za Wiliam kubadilika na kuachana na wanawake,zilienea kwa kasi ya moshi wa kifuu!Hapo ndipo akazidi kumpenda Wiliam,akamuwekea yeye ndiye atakuwa mumewe wa ndoa siku moja.Hakuelewa kwamba anacheza na joka la Mdimu,wakati wowote angemezwa na kutemwa jangwani.
Wiliam, hakuishia hapo,aliendelea kumfanyia Karishma maigizo,akawa anampeleka sehemu nyingi tofauti tofauti za starehe,Karishma akazidi kuwa mwenye amani na furaha,akadata!Akajiona amepata bonge la bwana.Hiyo haikutosha,Mtoto huyu Wiliam alikuwa ni mshenzi wa tabia.Kwani alitafuta wazee wawili mwanamke na mwanamme,akawalipa dola mia mbili kila mmoja ili waigize kama ni wazazi wake,jambo hilo likawa rahisi kwake.Akazidi kumsogeza Karishma karibu zaidi na kumjaza kingi.
“Nakupeleka ukawaone wazazi wangu leo”
Siku hiyo Wiliam alimwambia Karishma,ambaye alionekana kustaajabu mno!
“Hapana Raphael,ni mapema mbona”
“Nakupenda,ndio maana.Naomba kajiandae tafadhali,mimi naenda kuvaa”
“Lakini Mpenzi….Sawa ngoja basi nikajiandae”
Karishma akawa vuguvugu,sio baridi sio moto!Kifupi alikuwa sitaki nataka,ilhali moyoni alijawa na furaha iliyozidi kifani,kutambulishwa kwa Wazazi wa Wiliam lilikuwa jambo zito sana kwake ndiyo maana moyo wake ukachanua kwa tabasamu,ingawa mapigo yake ya moyo yalikuwa yakigonga kwa nguvu.Hakutaka kupoteza wakati,akanyoosha mpaka Hostel na kuanza kukagua ni nguo gani ya heshima zaidi aivae siku hiyo akienda ukweni!Kazi yake siku hiyo ilikuwa ni kuchambua kabati zima,akatoa nguo zote nje!

***** ****
“Nitakuja leo jioni mzee!Panga vitu vizuri hapo,hiyo picha niliyokupa.Itundike ukutani.Ukifanya vizuri nakuongeza dola nyingine Mia..Sawa sawa!Ahsante”
Wiliam alikuwa simuni,anaongea na Mzee Resty,babu ambaye alimpanga wafanye igizo hilo ili azidi kumsogeza Karishma karibu zaidi.Zoezi hilo lilionekana kuwa rahisi sababu nguvu ya pesa ilitumika.Nusu saa baadaye akawa tayari amejiandaa,akaenda kumfuata Karishma, ambaye alikuwa tayari amejipara,siku hiyo alipendeza kisawasawa!Wote wakaongozana na safari ya kuelekea Mandelbrodsvagen ikaanza, mji ambao Mzee Resty aliishi na mkewe!
Safari yao iliwachukuwa zaidi ya masaa mawili kwa gari mpaka kufika eneo hilo, ambapo walizidi kuingia ndani ndani.Huko wakakumbana na geti fupi la mbao!Pembeni kulikuwa na nyumba kubwa kiasi lakini iliyoonekana kuchoka kidogo,Wiliam akaingiza gari mpaka karibu na nyumba hiyo,akazunguka upande wa pili na kumfungulia Mlango Karishma!
“Karibu nyumbani mpenzi”
Wiliam,akasema!
“Mzeee Mzeee”
Wiliam akaita,akajifanya ni mwenyeji na kufungua mlango huku pembeni yake akiwa amemshika Karishma,wakazama mpaka seblen, ambapo huko wazee hawa waliopewa pesa wakajifanya kumchangamkia, Karishma.
“Mkwe karibu sana”
Bibi akasema na kumpa mkono Karishma,Mzee Resty nayeye akafuata!Karishma alijawa na furaha mno!Kazi yake ilikuwa ni kupepesa macho,ambapo ukutani aliona picha za Wiliam,nyingine akiwa mdogo nyingine mwanafunzi.Hilo likamfanya aamini kabisa!Kwa namna ambavyo mchezo ulivyochezwa kwa umakini, ilikuwa vigumu kugundua ya kuwa kila kinachotokea ni gelesha!
“Baba na Mama yangu kama nilivyowaambia!Huyu ni Mke wangu mtarajiwa,nampenda sana!”
Wiliam,akaanza kuongea kwa adabu zote huku akiwatizama wazazi wake, feki.
“Sawa sawa Mwanangu,umefanya jambo la maana sana!Na siku hizi magonjwa ni mengi,nashukuru kwa kunionesha heshima hiyo”
Mzee Resty kama angepewa nafasi ya kuigiza Bongo Movie,hakuna muigizaji yoyote yule angemfikia.Hiyo ni kutokana na namna ambavyo alivyokuwa anaigiza,hakukecha.Alizungumza kama baba mzazi wa Wiliam.Baada ya mazungumzo ya hapa na pale kuisha,wakaingia mezani na wote wakala kwa pamoja.
Sio siri, siku hiyo Karishma alifarijika kupita kaisi,akauhaidi moyo wake yakuwa angempa Wiliam zawadi nzito mno!
“Nitakupa zawadi kubwa sana,hutoamini”
Karishmna akamwambia Wiliam,wakiwa njiani ndani ya gari wanarudi.
“Zawadi gani?”
“Usijali”
“Niambie mpenzi”
“Nitakwambia na utaiona siku ikifika”
Zawadi hiyo ilikuwa ni kumvulia nguo yake ya ndani amkabidhi mwili wake,afanye naye ngono.Akiamini kwa kufanya hivyo atamfurahisha sana Wiliam ambaye kwa muda mrefu, alikuwa akiupigia misele mgodi wake,auchimbe!Lakini hakutaka kuliweka jambo hilo wazi!

*******
Mapenzi ya Wiliam na Karishma yalizidi kupamba moto,mara ghafla wakageuka na kuwa kumbikumbi kwani kila sehemu waliongozana pamoja,Karishma hakumpa nafasi Wiliam, azungumze na msichana yoyote yule,alijisikia wivu mno!Kifupi alikaba mpaka penati,Wiliam alivyoona Karishma yupo kohoni kwake namna hiyo, ilibidi simu yake aiweke ‘Silent’Muda wote, sababu bado alikuwa akipigiwa na michepuko yake mingine.Siku zote mwanamme hachungwi na ni mfano wa bahari,ukilinda huku wenzako wanavua kule.
Huyu ndiye alikuwa Wiliam,alikuwa ni mjanja kuliko Sungura.Ilikuwa ni lazima usiku atoke,akafanye ngono na wanawake zake baada ya kuagana na Karishma!
“Mpenzi,usiku mwema”
Kama kawaida yao,siku hiyo waliagana wakanyonyana ndimi.
“Nawewe pia mpenzi”
Hapo waliagana na Karishma alihakikisha Wiliam anazama chumbani kwake ndipo nayeye anaenda kulala.Lakini haikuwa hivyo malaya huyu, alikuwa akiamka usiku wa manane!Na kutoka nje,hiyo ndiyo ilikuwa mida yake ya kufanya uasherati kisirisiri.

******
Siku zilizidi kukimbia mithili ya maporomoko ya maji,mwishowe zikabaki siku chache ili wafanye mitihani ya kufunga chuo,Karishma akaonekana kuwa bize sana!Alikichimba kitabu kupita kiasi!Hatimaye mitihani ikaisha na kila mtu alitakiwa kurudi likizo!
“Mimi narudi Tanzania Mpenzi wangu”
Karishma siku hiyo, alimwambia Wiliam wakiwa kitandani.
“Nakutakia safari njema,jichunge sana huko.Ipo siku nitakuja kukutembelea!”
“Lini?”
“Likizo ikianza,nitakuja tu.Tuna likizo ndefu sana,miezi mitano!”
Baada ya kuongea hivyo,Wiliam akaanza kumpapasa Karishma,hesabu zake zilikuwa siku hiyo ajaribu kufanya naye ngono lakini jitihada zake, zilionekana kugonga mwamba,kwani Karishma alilalamika kuwa kichwa kinamuuma.
“Sawa”
Wiliam,akajibu lakini hakuonesha kufurahishwa!
“Usijisikie vibaya mme wangu!Mimi ni wako,naomba nikuhakikishie.Tukifungua chuo,nataka unitoe bikra yangu”
Karishma alimaanisha,alikuwa yupo tayari kumvulia Wiliam nguo sababu mpaka hapo alimuhesabia,ndiye angekuwa mmewe wa ndoa!Wiliam akaitikia kishingo upande,wakaishia kupigana madenda!

*******
Issa na Dokta Katrina siku hiyo walikuwa katika hekaheka kubwa,jioni hiyo ya saa kumi na moja!Ilikuwa ni lazima wafike uwanja wa ndege wa kimataifa Mwl.Nyerere saa 4;45 Usiku, ili kumpokea mtoto wao wa pekee Karishma!Ndiyo maana, siku hiyo waliwahi nyumbani na kujiandaa.
“Kuna foleni ya Tazara pale,sijui kama tutawahi”
Dokta Katrina,alikuwa anavaa huku akimwambia mmewe Issa, ambaye hata yeye alikuwa katika hekaheka hizo za kujiandaa!
“Tutawahi bwana”
“Si unamjua Yule mtoto kwa kununa”
“Tabia hizo si karidhi kwa Mama yake”
“Nani?Mimi?”
“Kumbe nani?”
“Labda baba yake”
“Huoni aibu”
“Baby fanya haraka,funguo za gari ziko wapi?”
“Gari gani?”
“Range”
“Seblen kule”
“Mafuta yapo?”
“Sidhani kama yatatosha,kwenye Vx ndiyo kuna mafuta”
“Basi tutumie Vx”
“Sawa,ilimradi tufike”
Dokta Katrina na Issa walikuwa wakijadiliana kuhusu safari hiyo na gari gani watumie ili kufika uwanja wa ndege kumpokea mtoto wao Karishma, ambaye alikuwa akitua na shirika la ndege ya KLM,siku hiyo walikuwa wenye furaha sana!Hawakuwa na muda wa kupoteza kwani baada ya kujiandaa,Issa akabeba funguo na wote kuingia ndani ya gari, ambapo safari ya kwenda Kipawa ilianza mara moja!Kutokana na msongamano wa magari,iliwachukuwa lisaa limoja lizima kuingia Uwanja wa ndege,wakapaki vizuri na kushuka.Moja kwa moja, wakaelekea kwenye viti maalum vya watu, wanaosubiri ndugu,jamaa na marafiki zao!Ndege haikudanganya hata kidogo kwani saa 4;45!Kipaza sauti kilisikika yakuwa KLM imetua,hapo Issa na Katrina walisimama na kuelekea langoni!Wakasubiri dakika kumi nzima,ndipo walipomtia machoni Karishma!
“Daaaaaaaaad!”
Karishma akaonekana kuwa mwenye furaha,akiburuza mabegi yake mpaka kwa wazazi wake!Wakakumbatiana,kwa furaha kukutana nao tena, uzuri wakiwa pamoja wenye furaha!
“Pole na safari.How was the trip Darling?”
Dokta Katrina akatupa swali,akichanganya na kimombo ili kuweka msisitizo!Akimaanisha safari ilikuwaje,maongezi ya furaha yakazidi, wote wakaingia ndani ya gari na safari ya kurudi nyumbani kuanza mara moja!

*******
Abraham,alibaki kuyatumbua macho yake kama mjusi aliyebanwa na mlango,mudi yake yote ikawa imekata,stimu imemtoka, hiyo ni baada ya kusoma ujumbe kutoka kwa mpenzi wake akimtaarifu ya kuwa, hatofika tena eneo la tukio ili wafanye ngono,ghafla akasinyaa!Hapohapo,akachukuwa simu na kumuendea hewani.
“Mbona sikuelewi?”
Abraham,akauliza simuni akiwa na jazba kidogo!
“Hunielewi kivipi Darling?”
“Una maana gani kuniambia hauji,si ungeniambia mapema Janeth ili nifanye mambo mengine”
“Sio hivyo Darling”
“Kumbe nini?”
“Baby,nipo getini kwenu hapa.Njoo unifungulie,nilikuwa nakutania.Njoo nje hapa nipo getini”
Mapigo ya moyo ya Abraham,yakapiga sambasoti!Hakuelewa kama ni kweli ama Janeth,anamzingua.Hapohapo akatembea akiwa na simu sikioni.Akatoka nje,mpaka getini!Akalifungua,akatabasamu baada ya kumuona Janeth,akiwa amependeza,ananukia marashi.
“Karibu Baby”
Abraham akasema huku akiweka simu yake mfukoni,akiwa anamtizama Janeth mambo yake ndani ya zipu, hayakuwa vizuri kwani nyoka wake alikuwa tayari amesimama dede,akatamani apae wakati huohuo wawe kitandani,hiyo ilitokana na akili kuwa tayari imebadilika.
Walivyoingia ndani,Abraham hakutaka kumkaribisha mgeni juisi wala maji,akamuingiza moja kwa moja chumbani kwake,akafunga mlango!Akamvuta karibu,akaanza kumnyonya mdomo,Janeth akawa nayeye hajiwezi tena,akatanua kinywa chake ulimi wa Abraham ukazama ndani,wakaanza kulana denda!Siku zote Abraham,huwa hakosei linapokuja swala zito kama hilo,mtoto huyu hakuwa mwenye papara kwani ndege alikuwa wake, isitoshe siku hiyo ndiyo ingekuwa mara ya kwanza kucheza mechi na Janeth,ndiyo maana hakutaka kutoa boko.Umakini ulihitajika,hapo ndipo alipoanza kuingiza mkono wake,taratibu ndani ya sketi ya Janneth,akakumbana na tumbo laini,akashuka chini zaidi,akaitoa sketi kidogo, akazidi kuingiza mkono ndani,mpaka alipokumbana na chupi!Akaipachua na kuanza kusaka kibuyu cha asali,kwa mbali akaanza kukichofya,Mpaka hapo Janeth hakujiweza tena!Akawa anapambana na hali yake,alichofanya nayeye hakutaka kuwa mzembe,akachukua mikono yake na kutumbukiza ndani ya suruali ya Abraham, ambao huko alikutana na nyoka mkubwa,akamtoa!Mpaka hapo Janeth akakosa stamina za miguu,akamsukumiza Abraham kitandani,puu!Akapanda juu yake,akamshika nyoka vizuri na kujaza mate mengi mdomoni,akamtumbukiza kinywani!Akawa anamlamba kama koni!



“Mpaka wangu mpaka huku,unaona hii alama hapa?Ndio mwisho wa shamba!Ukija kwa huku,mpaka kule mwisho.Hizi ni heka mbili,hapa Kwa Abraham atakuja kujenga nyumba yake na kule ni kwako!Hata nikifa kesho,mjuwe hicho kitu”
Deo Karekezi na mkewe Marietha, walikuwa tayari wamefika Korogwe!Niya ya Deo, ilikuwa ni kumuonesha mkewe kila kitu anachomiliki, kuanzia viwanja mpaka hostel za wanafunzi anazojenga,alikuwa mwenye kila sababu ya kufanya hivyo sababu aliamini kuna kesho na keshokutwa!Na ilikuwa ni lazima mkewe ajuwe kila kitu anachomiliki.Kazi ya kuzunguka eneo hilo haikuwa rahisi,kwani Deo alinunua eneo kubwa!
“Hapa napo nitajenga hostels pia,gorofa nne kwenda juu”
Deo akazidi kumwambia mkewe Marietha,ambaye alionekana bado vitu anavyoonyeshwa ni mazingaombwe,haikuwezekana hata kidogo kuamini kwamba Deo wakati anazungumza naye ndiye yeye, anamiliki mali zenye thamani, wakati alivyotoka jela,alikuwa ni kapuku tu hana kitu hata kimoja.Hana mbele wala nyuma,akatamani kuuliza lakini aliogopa kumtonesha Deo vidonda,ndiyo maana akaendelea kupiga kimya huku akishangaa ujenzi unavyoendelea kufanyika.
“Hongera sana Mme wangu”
Hatimaye akampongeza mmewe, akiwa katika hisia kali sana.
“Ahsante,nataka pia nikanunue shamba lingine kule nyuma.Kuna mzee mmoja ameniambia anauza”
“Sasa yote hayo?Ya nini?”
“Mke wangu,kwenye ardhi kuna pesa nyingi sana!Asikudanganye mtu!Next time, inabidi pia Abraham aje aone,twende naye Bukoba pia!Hata wewe hujawahi kufika”
“Kwenye mashamba yako?”
“Ndio,nina mashamba ya Mazao huko.Twende lini?”
“Mimi siku yoyote”
Hakukuwa na kipingamizi chochote,wote wakaanza kutembea na kuzunguka huku na kule, hatimaye wakamaliza heka tatu nzima!Marietha akawa yupo hoi bin taaban, anahema!
“Huku kote pia kwako?”
Marietha akaibua swali lingine huku akishangaa bonde,bado kulikuwa na kichaka kilichokuwa na miti na majani.
“Hapana,mpaka wangu unaishia hapa”
Kila kitu siku zote katika maisha kina historia,mfano ungepewa historia ya watu hawa wawili vitu ambavyo walipitia ungebisha,hakika walipitia changamoto nyingi.
“Sema nini Marietha….”
Deo akawa ana kitu anataka kukisema wakiwa wanatembea, kuelekea usawa wa gari lilipo.
“Nini tena?”
“Tumetoka mbali ujuwe”
“Saaaana”
“Lakini,siku ambayo ulinitisha ni siku ile uliyoniweka lockup”
“Ni hasira,nilipaniki.Au nawewe umesahau,ulivyokuwa unanipiga kama mpira na yule awara wako naniii sijui,Leila!Yaaani wewe mwanaume wewe?Hivi Leila yupo wapi?”
“Umeanza sasa”
“Wewe ndio umeanza,mimi namaliza.Tuachane na hayo Leila yuko wapi siku hizi?”
“Uingereza,sasa ana watoto mapacha!Na ndiye aliyenisaidia kipindi nipo gerezani”
“Mmmh,mlikuwa mna yenu nyie”
“Wala,Yule ni kama dada yangu”
“Nenda zako.Huna hata aibu mtu mzima mwenzio, unanidanganya mchana kweupee”
Hawakuwa siriazi,walikuwa wakizungumza kwa amani huku wakitaniana,wakaanza kukumbushana changamoto walizopitia na maisha yao kwa ujumla.
“Hivi Baba Abraham,umenipendea nini?”
Marietha akaibuka na swali zito,hiyo ilimfanya Deo amuangalie kwa kitambo kidogo!
“Vitu vingi tu”
“Bado mpaka leo,nimeshindwa kukuelewa.Kwa vitu vyote nilivyokufanyia ukanisamehee”
“Hapana,kwani mimi mangapi nilikufanyia?”
“Mengi,lakini hujanijibu swali langu.Kwanini umenipenda?”
“Nitakwambia,leo tusirudi Dar nataka tulale hukuhuku”
“Na Abraham atabaki na nani?”
“Keshakuwa mwanamme,atabaki peke yake.Mpigie simu kuwa tutalala huku,awe makini”
“Sawa”
Haukuwa utani,hapohapo Marietha alichukua simu na kumtafuta Mwanaye Abraham hewani,akamueleza kila kitu kilivyopangwa!Walivyoingia ndani ya gari,wakaenda kukodi hotel ambapo huko baada ya kuingia tu,wakaanza kunyonyana ndimi kwa fujo,kila mtu alionekana kuwa mwenye furaha!Siku zote Ng’ombe mzee hazeeki maini,kwani Deo alionekana bado ni fundi kitandani,alimsogeza Marietha na wote kuingia kitandani kushiriki tendo hilo ambalo lilihalalishwa kwa wanandoa hao!

*********
Kwa Abraham siku hiyo ilikuwa kama sherehe,baaada ya kupokea simu kutoka kwa Mama yake ya kuwa hawatorudi jijini Dar es salaam!Akatamani kupiga yowe la nguvu,hiyo yote ilitokana na tukio alilokuwa analifanya na mpenzi wake Janeth,akakenua meno yake yote nje!Akapata nguvu mpya nyingine, baada ya kutoka kufunga goli la kwanza.Bila kusema kitu kingine chochote kile,akamsogelea Janeth mdomoni na kuanza kumla denda,mtoto huyu hakuishia hapo!Alifuata taratibu zote za mchezo huo, ambao hauhitaji hasira,akachimba madini ya kutosha,akapiga mashuti ya mbali.Kelele za puani alizokuwa anatoa Janeth zilizidi kipimo chake,kwani Janeth alilalamika huku akiwa anataja jina la Abraham.
“Abraaaam aaaah assshhh aaaah baaasi,aaah yeeees”
Hiyo ndiyo miguno ya puani aliyokuwa anatoa huku akiwa chini,anamkwaruza na kucha zake, zilizokuwa ndefu kiasi,hali aliyokuwa anahisi ilizidi kipimo chake!Hatimaye mechi ikawa imekwisha,Janeth akawa hoi!Jasho kwa mbali linamtoka.
“Washing room ni wapi?”
Janeth,akamuuliza Abraham wakiwa wamejifunika, shuka moja!
“Hapo”
“Okay nakuja, naenda kususu”
“Aya baby,nakusubiri”
Kila kitu kikaonekana kuwa ni ushindi mkubwa kwa Abraham,akabaki anamtizama Janeth, anavyotembea akiwa hana nguo hata moja, akielekea bafuni kwenda kutoa haja ndogo,bado hakuamini kama ametoka kufanya tendo hilo na msichana huyo mbichi!
“Baby,I’m back.Niambie sasa”
Janeth akasema huku akiruka kitandani,akamfuata Abraham midomoni na kumnyonya ulimi.
“Nime enjoy leo Abraham,you are the best”
Janeth akatoa sifa.
“Hata wewe”
“Mimi nina nini sasa?”
“Una vitu Fulani,amaizing”
“Ha!Haa! Haaa! Haaaa! Haaa!”
Kila kitu kilionekana kuwa furaha kwa wawili hawa,Abraham alianza kumpenda kweli Janeth!Siku hiyo, walizungumza vitu vingi sana, hususani uhusiano wao utakavyokuwa,wakadiriki kwenda mbele zaidi na kuhaidiana ya kwamba siku moja watafunga ndoa na kuzaa watoto!
“Nikuzalie watoto wangapi,nikiwa mkeo”
“Hata mia moja”
“Khaaa!Nimekuwa Nguruwe”
“Hahahaha,basi wanne tu”
“Hapo kidogo sawa,sipati picha watoto wetu watakavyokuwa”
“Kwanini?”
“Watakuwa wazuri mno”
Waliendelea kuongea vitu vingi sana na kuzidi kulipigilia penzi lao misumari,kwa kuwa siku hiyo wazazi wa Abraham walisema hawatorejea hivyo walikuwa na kila sababu ya kujiachia watakavyo,wakaona chumbani hapatoshi!Wakaenda Seblen,huko hawakukaa hata sekunde moja,wakaanza kutekenyana mwisho wakaishia kunyonyana midomo na kutomasana,kilichofuata hapo!Wanajuwa wao wenyewe.
********

Kila kilichotokea kwa Karishma kilikuwa kama ni muujiza mkubwa sana kwani yeye kujiingiza kwenye mahusiano ya kimapenzi lilikuwa ni jambo gumu kwake,hata siku moja hakuwahi kuota ama kuwaza kama atakuja kupenda na kuoza namna hiyo na ujanja wake wote wa kuwachomolea wanaume wenye nguvu za pesa na maarufu, lakini alijikuta amenasa kwenye tundu bovu, baada ya kuzama katika penzi la Wiliam,mwanamme shombeshombe!Haukuwa uchawi wala ndumba,Karishma alikufa na kuoza kabisa,kila mara Wiliam akawa ndani ya kichwa chake, akatamani awe karibu naye kila sekunde.Alitamani kuwa mwenye uwezo wa kusogeza siku mbele ili chuo kifunguliwe, akaonane na barafu wa moyo wake,lakini hilo lilishindikana!Kilichokuwa kina mfariji kwa kipindi hiko kigumu ni mawasiliano ya simu,Karishma hakuweza kupitisha sekunde moja bila kumtumia meseji Wiliam kwa kupitia mtandao wa ‘WatsApp’.Waliongea na wakati mwingine kupigiana Skype usiku,wakionana uso kwa uso!Karishma akafarijika,akawa analala kwa amani na furaha.Siku zikazidi kusonga mbele!

******
“Uwe unatoka nawewe,uwe unatembea mwanangu Mungu akuone,usipende kukaa kaa ndani, kama utumbo”
Siku hiyo Dokta Katrina akamuibukia Karishma chumbani kwake,akimpiga vijembe kwani tangu alivyopata likizo hakuwahi kutoka nje hata siku moja!
“Sasa Mama nitaenda wapi?Sina rafiki yoyote”
“Kazunguke zunguke hata Shopprite.Kama unapenda kukaa ndani,sawa!Ni maamuzi yako”
Kitu kama hicho Karishma kilimshtua mno,hakutegemea kama Mama yake angemruhusu atoke nje kienyeji kwani siku za nyuma alikuwa akilipiga vita, jambo hilo kuliko kawaida.
“Basi Mama Kesho nataka kwenda Kigamboni,Beach”
“Unapajua?”
“Ndio”
“Utaendaje sasa?”
“Nitapanda daladala”
Kila kilichotokea kwa Karishma kilikuwa bado anakitafsiri kama ni mazingaombwe,ndio maana alikuwa akimjibu Mama yake kwa wasiwasi kuliko kawaida.
“Nitakutafutia mtu,akupeleke”
“Sawa Mama”
Siku hiyo Karishma bado hakuamini,alitegemea Mama yake baadaye angeingia tena chumbani kwake na kumuambia kuwa ‘Hakuna kutoka,nilikuwa nakutania’Lakini haikuwa hivyo.
Siku iliyofuata alidamka asubuhi na mapema na kupata kifungua kinywa,dakika kumi baadaye alifika dereva ili amuendeshe na kumzungusha sehemu yoyote anayojisikia kwenda. Karishma kwa siku hiyo,alijifananisha na ‘First lady’ yaani mke wa Rais,kwani kila alipomuamuru dereva aweke gari kando,ndicho kilichotokea!Saa saba mchana wakawa wapo juu ya Pantoni ili kuvuka upande wa pili kuelekea Kigamboni.
“Ukivuka hapo,simama stendi nataka nikanunue maji ya kunywa”
Karishma akamwambia dereva na hicho ndicho kilichoenda kufanyika.Baada ya gari kuvuka kutoka juu ya pantoni, dereva akatafuta paking nzuri na kuliweka gari kando, pembeni mwa duka kubwa ambapo nje kulikuwa na wateja wengi wamejaa,wakitaka huduma!
“Nakuja kaka,sasa hivi”
“Nakusibiri”
Dereva akajibu!Karishma akaweka miwani yake ya jua machoni,akatembea hatua chache mpaka dukani.
“Nipe na hizo karanga”
Ni sauti ambayo Karishma aliisikia ikitokea mbele na haikuwa ngeni katika masikio yake,akajaribu kuvuta kumbukumbu ni wapi aliisikia lakini hakupata jibu la harakaharaka.Mpaka kijana huyo alipogeuka,haikujulikana kama Karishma alishtuka au aliogopa sababu mapigo yake ya moyo yalipiga kwa nguvu mno,akabaki ameduwaa!
“Abrahaaaam”
Akajikuta ameropoka bila kutarajia.Hakumfananisha hata kidogo,mbele yake alisimama Abraham akiwa amependeza kuliko kawaida,Karishma akahisi kuishiwa nguvu!Mapigo yake ya moyo yakabadili mwendo,akashindwa kuongea chochote.Bado uzuri wa Abraham ulikuwa wa kipekee, machoni mwake.
“Abraham,niwewe kweli?”
Akauliza kwa mshangao.
“Ndio mimi,mambo vipi?”
Hapohapo Karishma akavua miwani.
“Abraham,where have you been?”(Abraham,ulikuwa wapi)
Karishma akauliza kwa hisia za waziwazi huku akimtizama Abraham machoni!
“Nilikuwa around”
“Unafanya nini huku?”
“Nimekuja kumuona rafiki yangu,anaishi vijibweni”
“Anywei,naomba namba zako za simu”
“Poa”
Abraham hakuwa na hiyana,akatoa namba za simu kisha kuondoka zake huku nyuma akimuacha Karishma akimsindikiza kwa macho!
********

Karishma,Mara ghafla akageuka na kuwa kama ndumi la kuwili.Moyo wake ukajikuta unatamani tena kuwa na Abraham kimapenzi,japokuwa kwa mara ya kwanza alijizuia.Alijilazimisha kumtoa kichwani ili atulie na mpenzi wake Wiliam lakini kwake zoezi hilo likaonekana kuwa zito mno!Meseji walizokuwa wanatumiana na Abraham zilizidi,mpaka usiku walitakiana usiku mwema!Kilichomvuruga zaidi Karishma ni sauti ya Abraham,ambayo alikuwa akizungumza taratibu kwa mapozi na bezi lake zito kiasi.
“Poa usiku mwema.Nasikia usingizi,naomba nilale Karishma”
Siku hiyo walitia fora kwani walizungumza mpaka mida ya wanga,saa tisa za usiku.
“Abraham,naomba nikwambie kitu kimoja”
“Kitu gani?”
“Naumia kwa ajili yako”
“Kivipi?”
“Nakupenda Abraham,sijui kwanini.Naomba nikubalie,nitajiita mwenye bahati”
Karishma alizungumza maneno hayo,ambayo kwake hakuwahi kuyasema tangu azaliwe!Mbali na hapo,alikuwa ni msaliti mkubwa.Kifupi alikuwa akijaribu kupanda farasi wawili kwa wakati mmoja.
“Nina mpenzi tayari”
“Sawa,lakini nitakuonesha kuwa nakupenda sana.Nipe hiyo nafasi Please please”
“Nitaamini vipi,unanipenda?”
“Nipe nafasi ili ni prove”
“Sawa,usiku mwema”
“Abraham,unanipenda?”
“Nimekupa hiyo nafasi”
Moyo wa Karishma ukapiga kwa nguvu,hakuyaamini masikio yake hata kidogo!
“Nakupenda Abraham,nakupenda sana!Mwaa mwaaaa!”
Hatimaye,Karishma akawa ameingia kwenye mkataba mwingine wa mapenzi na Abraham!




Hatimaye,Karishma akawa mwenye furaha kuliko kawaida.Kukubaliwa kimapenzi na mwanamme ‘Handsome boy’ kama Abraham baada ya kumfukuzia kwa kipindi kirefu, kwake aliijita mwenye bahati ingawa alikuwa ana mpenzi tayari anayeitwa Wiliam,kwake hilo hakujali japokuwa alimpenda pia.Tangu Abraham awe naye, kuanzia siku hiyo maisha ya Karishma yakabadilika kabisa,muda wote akawa mwenye furaha,anacheka mwenyewe!Moyo wake ulikuwa ukienda mbio kila simu ya Abraham ikiita,kitendo cha kioo chake cha simu kuandika ‘LOVE’mapigo yake ya moyo alihisi yanapiga kwa nguvu, ilikuwa ni lazima atabasamu kwanza kabla ya kuiweka simu sikioni.
“Yes Daaaarling”
Siku zote Karishma hupokea simu ya Abraham kwa mbwembwe!Na kuanzia hapo, siku zote Abraham alikuwa akiitwa majina ya kimahaba.Kama Darling,Love,Honey,Sweatheart,Amore,ini mkalia nyongo na mengine kibwena, ilimradi vurugu tupu,sio siri alijihisi ni mtu wa tofauti mno.
“Unafanya nini now?”
Abraham akauliza simuni.
“Nilikuwa nakuwaza wewe,ndio ukanipigia”
“Unaniwaza mimi?Kwanini?”
“I can’t wait, to see you”(Sipati picha,nikikuona)
“Oh,hata mimi”
“So,lini Honey?”
Karishma alikuwa mwenye kiu ya kumuona Mpenzi wake huyo, Abraham.
“Siku yoyote ile,lini upo free?”
“Wewe sema”
“Jumamosi”
“Jumamosi?Ipi hii?”
“Yes”
Kama kawaida ya Abraham,siku ya Jumamosi anakuwa anajuwa ya kuwa anaachiwa jumba peke yake,nafasi hiyo ndiyo huitumia bila makosa yoyote yale.
“Wapi?”
“Home”
“No baby,Home?What about wazazi wako?”
“Hilo niachie mimi”
“Are you sure?”(Una uhakika)
“Yah”
Tangu siku hiyo, Karishma akapata kizungumkuti,siku kwake zikawa zinaenda kwa mwendo wa ajuza.
Sio siri hakuelewa ni kitu gani kinamsukuma namna hiyo,kazi ya moyo wa Karishma haikuwa tena kusukuma damu, bali penzi la Abraham,kichwa kizima kilitawala Abraham!Mbaya zaidi walianza michezo michafu ya kutumiana picha,kwa nguvu ya penzi Karishma akasahau maadili ya dini yake,akawa anamrushia Abramam picha za nusu utupu, akiwa katika vazi la kulalia yaani ‘night dress’kwa upande wake binafsi alijiona yupo sahihi kabisa akiamini kwamba hayo ndiyo mapenzi.Simu yake ikawa imejaa picha za Abraham,akaenda mbali zaidi na kumuweka ‘screensaver’Juu ya kioo cha Karishma alijaa Abraham,akawa kila wakati anaitizama simu yake ili amuone Abraham.
Penzi lake lilikuwa ni sawa na mzani huku Abraham kule Wiliam,kadri siku zilivyozidi kwenda mbele mzani wa upande wa Wiliam ukawa unashuka taratibu,hilo halikupingika sababu alimpenda sana Abraham!Mapenzi kwa Wiliam yakaanza kupungua kwa kiasi cha kutosha,mara ya kwanza alikuwa akipokea simu yake kwa kujifikiria lakini siku zilivyozidi kwenda mbele,akawa hapokei kabisa,hilo lilimfanya Wiliam aanze kuhisi tayari penzi lake limechacha kwani hakuwa mgeni wa wanawake,alivurugika kupita kiasi kwani alitumia nguvu nyingi sana kumuwinda mtoto huyo mrembo,machale yakaanza kumcheza akatamani siku moja aibuke Afrika,nchini Tanzania ili akaonane uso kwa Uso na Karishma amuulize kulikoni,swala la kusafiri mpaka Afrika kwake alilifananisha na ndoto,ilikuwa ni lazima itimie.Ndiyo maana akaanza kusuka uwongo kichwani ili awaeleze wazazi wake.

***** ****
Karishma alikuwa tayari amenasa kwenye ulimbo na ujanja wake wote ukawa mfukoni,hakusema lolote juu ya Abraham,akawa ametulia kama maji mtungini.Siku ya Jumamosi ndiyo ilikuwa siku waliyopanga waonane!Siku hiyo Karishma ilijipamba sio kitoto,asubuhi ya siku hiyo akamtafuta hewani rafiki yake wa kike ili azuge kwamba anaenda kwake,hivyo ndivyo hata mama yake alimdanganya pia!Haikuleweka ujanja huo aliubuni kutoka kwa nani, lakini ndivyo walivyopanga na rafiki yake anayeitwa Muzdalfat.
“Sikia Muzdalfat,Mom anajua nakuja kwako!Nitakuja hapo,alafu nitakwambia cha kufanya”
Karishma alikuwa akipanga na rafiki yake simuni,yupo chumbani tayari keshapigilia pamba za kwenda kuonana na kidume, Abraham!
“Sawa,njoo Tutaongea”
“Okay,see you soon”
Hata ingekuwaje,isingewezekana kwa Karishma kuruhusiwa kutoka mwenyewe ndani ya jumba hilo bila ya dereva,ndiyo maana alitaka hatua ya kwanza aikamalishe kisha mengine yafuate!Alivyohakikisha kila kitu kimekaa sawa,akatoka na kuwaaga wazazi wake ambao, walikuwa seblen.
“Utarudi saa ngapi?”
Issa akauliza.
“Kabla ya saa kumi Dad”
“Uwahi kurudi,kuna foleni”
“Sawa Dad,Mom baadaye”
“Sawa Karishma”
Wazazi wake hawakuelewa kwamba wanapigwa changa la macho kwani Karishma, alikuwa ana mipango mingine kabambe,akatoka mpaka nje ambapo huko aliingia ndani ya gari.Dereva akawasha gari,safari ikaanza hapohapo!Haikuchukuwa muda mrefu sana, kutokana na barabara kuwa nyeupe,magari machache.Wakawasili Kigamboni,wakafika mpaka Mji Mwema!
“Kata kulia”
Karishma kuanzia hapo akaanza kutoa maelekezo,dereva hakuwa na tatizo kwani alikuwa akimuendesha mtoto wa tajiri yake,hata kama angemwambia liingize gari ndani ya bahari angefanya hivyo,kwake mtoto huyo alimfananisha na mtoto wa Rais,sababu kwa kazi hiyo tu,alilipwa mshahara mnono!Alivyozungusha usukani akapewa maelekezo, mengine!
“Kwenye ule mtaa,utaingia kushoto”
“Sawa”
Alichotaka Karishma kiwe,ndicho kilichotokea kwani walifika mpaka nje ya geti la rangi ya kijivu.
“Mimi nimefika,unaweza ukapaki gari kule kona.Nitakukuta”
Baada ya kutoa maagizo hayo,Karishma akateremka kutoka garini, akatoa simu yake na kumtafuta Muzdalfat hewani.
“Nipo getini,njoo”
“Poa”
Dakika moja ikawa nyingi,akatokeza mrembo kutoka ndani ya geti, mwenye rangi ya maji ya kunde.
“Mimi sina muda wa kupoteza,Muzdalfat.Nataka niende Upanga sasa hivi”
“Kwa nani tena?”
“Kuna mtu naenda kumuona,lakini Mama akikupigia, mwambie nipo nawewe”
“Sasa akitaka kuongea nawewe?”
“Hawezi kufika huko,nielekeze.Nataka kufika Upanga,nipande magari ya wapi?”
“Ukifika Posta,tafuta magari ya Muhimbili.Ama Kariakoo.Ukipata Muhimbili,shuka Azania kisha uulize mtaa unaotaka kwenda.Kama Kariakoo Pale Msimbazi, alafu chukua bajaj”
“Sawa,nitarudi sasa hivi.Hii ndiyo Golden Chance nimeipata”
Karishma hakutaka kupoteza wakati asubuhi ya siku hiyo,nafasi hiyo kwake aliifananisha na ‘Golden chance’ yaani nafasi ya dhahabu!Kila kitu kikaonekana kuwa bam-bam kwake,hakutaka kupanda daladala,alihofia kupoteza muda!Akatafuta pikipiki ambayo ilimpeleka mpaka Kivukoni,hapo alisimama ili kusubiri pantoni, limvushe upande wa pili!

*********
Siku hiyo Abraham,alikuwa akijishindilia asubuhi chakula cha kushiba,aliamini ya kuwa ni lazima angemvua mtoto huyo shombeshombe nguo yake ya ndani ili afanye naye ngono.Ndiyo maana alihakikisha anapiga msosi wa nguvu,akashushia na glasi ya maziwa,alivyotimiza kila kitu,akaingia chumbani kwake na kuanza kupanga,akatandika kitanda na kudeki chumba chake,kikawa kisafi kuliko kawaida!Kifupi siku hiyo, Mbuzi alifia kwa mpika supu,ilikuwa ni lazima aliwe mchuzi.Siku hiyo Abraham,alijifananisha na mpika Supu,Karishma ni Mbuzi.Kilichofanya akili yake ichachawe zaidi ni picha za Karishma alizokuwa amemtumia, amepiga na nguo ya kulalia!Picha za Karishma hazikumchosha kuangalia,wakati mwingine mwenyewe alikiri katika mademu wote aliowahi kutembea nao,Karishma alikuwa ni moto wa kuotea mbali.
“Huyu mtoto leo…Atanikoma!Hapa nimeshiba,ngoja nikaoge sasa”
Abraham,alizungumza mwenyewe huku akikiangalia kitanda chake namna ambavyo kilivyokuwa kikubwa!Akawa anajiona jinsi, atakavyokuwa kitandani na Karishma wanafanya tendo hilo la kuzini,alivyotaka kuingia bafuni simu yake ikaita.Alikuwa ni kama ametabiri vile kwani simu hiyo ilitoka kwa Karishma,akaipokea na kuiweka sikioni.
“Darling,nipo Kariakoo”
“Ndio unakuja?”
Abraham,akauliza swali la kijinga!Ilhali alikuwa akijuwa ratiba nzima ya Karishma.
“Ndio Love”
“Aya,kama nilivyokuelekeza”
“Sawa,lakini nachukuwa bajaj”
“Hakuna shida Baby”
“Aya mpenzi”
Kitendo cha Abraham,kukata simu.Kama mkuki,akazama moja kwa moja bafuni kujimwagia maji, huko hakutumia hata sekunde saba,akawa tayari ametoka!
Akajipulizia marashi,akavaa boxa mpya na kaptula.Akaweka na shati mwilini.Akabeba simu yake na kwenda kujitupa seblen juu ya kochi.Dakika nne zikawa nyingi,Karishma akawa tayari amempandia hewani,akimwambia amefika tayari kituo cha Azania!Alichofanya Abraham ni kuanza kuongea na dereva huyo wa Bajaj,akamuelekeza mpaka anapoishi.Maelezo yalivyokamilika dakika moja mbele,akasikia muungurumo wa bajaj nje ya geti,akajua tayari mambo yameiva.
“Ding dung”
Kengele,ikasikika!Abraham akasimama na kuweka shati lake vizuri,mpaka nje ya geti.Ambapo huko alikumbana na kisura,sio siri siku hiyo kwa Mara ya kwanza Abraham kupigwa na butwaa la waziwazi!
Ilikuwa ni wazi kabisa ya kuwa alishawahi kutembea na wanawake wazuri na wenye shepu kali, lakini kwa Karishma alizidi,ndiyo maana akabaki ameduwaa!Na haukuwa utani,Karishma alikuwa ni mrembo sio kawaida,rangi yake ilikuwa imechanganyika,ngozi laini mno.
“Oh,Karibu Love”
Abraham baada ya kuwa ameduwaa kwa kipindi kirefu,hatimaye akamkaribisha mpenzi wake ndani.Wote wakaingia ndani,Karishmna alivyotangulia mbele ya Abraham, ndiyo usiseme!Haikujulikana kama anafanya kusudi ama ndio mwendo wake,Karishma alitembea kwa mikogo na madoido,hakuelewa ya kuwa nyuma yake kuna Abraham ambaye, alionekana kuweweseka kuliko kawaida.
“Mmmmmh”
Abraham,akajikuta ameguna bila kupenda, hiyo ilimfanya Karishma ageuke nyuma.
“Vipi?Mbona umeguna?”
“Hujui kwanini nimeguna?”
“Ndio”
“Makusudi unanifanyia”
“Kivipi?”
“Hujui,ulichobeba.Hili umbo umerithi kwa nani?”
“Hata sijui”
“Mme mwenza anafaidi”
Hata siku moja,kwa uzuri aliokuwa nao Karishma haikuwezekana kwa Abraham kumuingia akilini ya kuwa, yupo peke yake,ilikuwa ni lazima atakuwa amewekwa mshkaki.Kuna msululu mwingine wa wanaume tena wenye nguvu ya pesa,wapo kimapenzi na Karishma.Ndiyo maana akasukuma msemo huo ili kupima maji.
“Mme mwenza kivipi?”
“Si mwenzangu,anayekuhudumia”
“Upo peke yako Abraham”
“Ah wapi,tuachane na hayo!Karibu ndani”
Walivyokuwa wanazungumza walikuwa wamesimama wima,Abraham akapita mbele na kufungua mlango,akamkaribisha Karishma ndani.Wote wakaketi juu ya makochi!
“Nakuletea juisi”
“Sawa mpenzi,wale ndio wazazi wako?”
Karishma akatupa swali, baada ya kupiga jicho juu ya ukuta na kuona picha za watu wazima wawili na katikati yao,akiwa Abraham.
“Ndio,Yule Baba yangu.Yule Mama yangu”
“Umefanana sana na Mama”
“Kweli?”
“Exactly”
Hapo Abraham,akaliendea friji na kutoa kopo moja la Juisi,akabeba glasi na kumimina!Akamkabidhi Karishma!
“Ahsante”
“Karibu tena”
Hapo wakaanza kuzungumza mambo ya hapa na pale,Abraham akaonesha kuwa muongeaji sana.Kadri stori zilivyozidi kunoga,ndivyo Abraham akaonekana kumsogelea karibu kabisa Karishma,akamshika kiuno na kumvuta karibu yake,akamnyang’anya glasi ya juisi akaiweka kando!Hapohapo,hakupoteza wakati.Akamsogelea mdomoni,kilichofuata hapo kama Karishma alikuwa akisubiria vile, sababu hata yeye alionesha ushirikiano kwenye zoezi hilo,wakaanza kulana denda!Kila mtu akasisimka,Abraham hakuishia hapo!Akapeleka mkono wake mmoja juu ya kifua cha Karishma, hapo ndipo mrembo huyo alipoanza kutoa miguno ya ndani kwa ndani.Akaanza kufumba macho, akahisi sketi aliyovaa inafunguliwa zipu,alitamani kuushika mkono wa Abraham lakini alihisi kuishiwa nguvu,sketi yake ikaanza kushushwa taratibu kwenda chini.
Haikufahamika ni kwa namna gani lakini alivyofumbua jicho lake moja,akagundua amebakiwa na chupi peke yake.Karishma akahisi aibu,akawa anamtoa Abraham ili asiendelee na zoezi hilo.Haikuwa kazi rahisi, sababu tayari alishaanza kuchemka,mbaya zaidi shingo yake ilikuwa inanyonywa!Hapo ndipo akazidi kuwa hoi.Akawa anahisi kama kuna wadudu wanatembea ndani kwa ndani,akawa hajiwezi tena!Abraham alivyotaka kuvuta chupi,ndipo alipoweka mgomo,akaushika mkono wa Abraham.Ghafla ikatokea vuta n’kuvute.Kwa ugwiji aliokuwa nao Abraham,hakutaka kufosi!Akaendelea kumtomasa vilivyo Karishma,akamnyonya shingo,akamtomasa kifua,na kumpapasa kila mahali.Hali aliyoanza kuhisi Karishma haikuwahi kumtokea tangu azaliwe,ndiyo maana akaanza kutoa miguno ya fujo, hapo ndipo Abraham,hakuremba!Akachojoa chupi ya Karishma!Yote mpaka chini,akajaribu kupima oil lakini wapi,hapo ndipo Karishma alipoanza kuhisi maumivu,akawa anajaribu kuutoa mkono wa Abraham bila mafanikio yoyote.
“Abra…aham naumiaaaaa”
Karishma alilalamika baada ya Abraham,kujaribu kupima oil kwa nguvu!Hilo lilizidi kumshangaza Abraham,lakini hakujali.Alikuwa tayari amepandisha mori,akasukuma kaptula yake na kuivua,ndizi yake ikawa nje.Kwa mara ya kwanza Karishma kuona uume ilimfanya azidi kutetemeka na kuhofia,akaanza kumsukumiza Abraham kwa nyuma,lakini hakuweza kushindana naye nguvu.Miguu ya Karishma ikashikwa huku na kule,Abraham akaseti mitambo,akaanza kuutafuta mgodi huo ambao ulikuwa mdogo mno!Abraham akawa anafanya kazi ya ziada kutumbukiza mashine ili uchimbaji uanze,hapo ndipo sekeseke lilipoanzia,Karishma akawa anapiga kelele huku anamsukumiza Abraham lakini wapi.
“Abraah….am please stoooooop”
Sauti yake haikufahamika kama ni kweli anaumia ama ni rahaa,hapo Abraham akazidi kusokomeza gunzi kwa ndani.Maumivu aliyokuwa anahisi Karishma hayakuwa na kipimo chake,akaanza kulia kama mtoto mdogo huku akilalamika Abraham atoke,kutokana na ukubwa wa ndizi aliyokuwa nayo Abraham,haikufikia hata nusu!Abraham akahisi kuna kitu kisichokuwa cha kawaida,akahisi ndizi yake imelowa!Alivyopiga jicho kwa chini akaona mapaja ya Karishma yamelowa damu nyingi,moyo wake ukapiga paa!Kwa nguvu.

********
“Ma..maaaa Naku…fa!Nisa…dieeee Ma…maaaa aargiiiii”
Damu zilikuwa zikimtoka kila mahali,sio kichwani wala puani kotekote mpaka tumboni.Hakukuwa na msaada tena zaidi ya kifo kibaya ambacho kingetokana na majeraha ya kupigwa risasi pamoja na kuchomwa chomwa na vitu vyenye ncha kali.Mbali na kuwa katika hali ya namna hiyo lakini aliweza kujiburuza kama nyoka na kuacha alama za damu kwa nyuma.
“Ma..maaa nisai..die”Huyo ni Abraham akiwa anaomba msaada,ni wazi kabisa alikuwa yupo mbioni kufa.Marietha alikuwa pembeni yake,kwanza alitamani kukimbia.Hakumtambua ni nani lakini, alivyotuliza akili yake na kumuona Abraham ndiye yupo nje ya geti.Akahisi nguvu zinamuishia,alivyotaka kumsogelea akaona mwanga wa gari, ambalo lilikuwa lina kuja kwa kasi upande wake wa Magharibi,gari hilo likapiga breki kandokando ya Abraham.Wakashuka wanaume wawili weusi kisha baada ya sekunde moja, akateremka kijana mmoja mwenye rangi ya mchanganyiko,akiwa ameshika bastola mkononi.Marietha alivyomuangalia vizuri usoni alishindwa kumtambua sababu ya mwanga kuwa hafifu kwa mbali.Hapo ndipo kijana huyo, alipoanza kumshambulia Abraham akitumia magongo makubwa huku akizungumza kwa lugha ya kiingereza!Marietha akaanza kupiga kelele za kuomba msaada lakini hakuna hata mtu mmoja aliyejitokeza kumsaidia,ghafla mlango wa gari hilo ukafunguliwa.Akatokeza mzungu mwenye nywele nyingi na ndevu chungu mzima chini ya kidevu chake,sura hiyo ilikuwa sio ngeni kwa Marietha lakini hakuelewa ni wapi,aliiona.
“William,kill him” (William muuwe)
Hapo ndipo Marietha alipopatwa na kumbukumbu, kutokana na sauti hiyo.Na jina Wiliam ndilo, likampa majibu ya maswali yake.
“Amadour”Hatimaye,akamkumbuka.
Huyu ndiye mwanamme aliyekuwa mkandarasi wa matatizo kutokea katika maisha yake,akakumbuka namna alivyobakwa ndipo akatokea mtoto Wiliam,akapandwa na hasira ajabu!
“Mariethaaaaaaa”Amadour,akaita.
Hakuwa tayari kuamini kama Wiliam yupo mbele yake, tena yupo mbioni kumuua kaka yake Abraham,mbaya zaidi Amadour nayeye alikuwa akimuunga mkono.Alivyotaka kuingilia,Amadour akachomoa bastola kutoka kiunoni.
“Paaaaaaaaaaaaa!”
Akafyatua,risasi ikamfikia Marietha moja kwa moja tumboni.


Abraham na Karishma,wapo ndani ya chumba kimoja.Wote wana vitambaa vyeusi usoni.Hakuna hata mmoja kati yao aliyekuwa anajua ni wapi alipo.Mpaka pale waliposikia mlango unafunguliwa,wote wakabebwa msobe msobe mpaka sehemu yenye uwazi.Jumba walilohifadhiwa lilikuwa kubwa lakini halikuisha,lilikuwa kama gofu.Ni chumba kimoja tu,ndicho kilikuwa kina mlango na haikuwa rahisi kwa mtu yoyote yule,kugundua kama ndani ya jumba hilo kuna chumba kidogo. Mbaya zaidi, eneo zima lilizungukwa na miti mirefu.Mbele ya uwazi huo,alisimama Wiliam,anawatizama Abraham na Karishma, waliokuwa na vitambaa bado!Akatoa ishara ya mkono vitambaa vitolewe.Butwaa,alilopigwa Karishma halikuwa na mfano wake,alishangaa mara mbili sababu mbele yake alisimama Wiliam na pembeni alikuwa Abraham,akahisi kutetemeka ajabu.Hata hivyo mchongo huo mzima alijua Wiliam ndio kaupanga.
“Bitch”(Malaya)
Wiliam akasema huku akibenua mdomo kwa dharau,akiwatizama Abraham na Karishma!
“You son of a bitch,do you remember this face?”(Wewe mtoto wa Malaya unaikumbuka hii sura)
Wiliam alimuita Abraham mtoto wa Malaya, bila kujua,huyo ni kaka yake na anamtukana pia mama yake vile vile.
“Let me tell you one thing.I DON’T STOP WHEN I’M TIRED.I STOP WHEN I’M DONE”(Ngoja nikwambie kitu,sisimami nikichoka.Nasimama nikimaliza)
“Please Raphael”(Tafadhali Raphael)
Karishma alianza kububujikwa na machozi,mbele yake alikiona kifo kwani alimuelewa vizuri sana Wiliam!
“Shut up, you hypocrite”(Nyamaza mnafki wewe)
Maongezi baina ya Wiliam na Karishma, yalivyokuwa yanazidi kuendelea ndipo Abraham alijuwa.Watu hao ni wapenzi na kila kitu kutokea siku za nyuma ufukweni,kilisababishwa na wivu.Abraham hakutegemea kama Karishma angekuwa kicheche namna hiyo,lawama zote akaanza kumtupia yeye.Akajuta kujiingiza katika mahusiano na Karishma.
“Broo…Mimi huyu nakuachia…Mimi niache niende kama demu mimi fresh mchukue”
Abraham alizungumza kwa niya ya kujitetea akiwa bado mwenye hofu.
“What are you saying?In English,I don’t speak your fucking language.I’m gona kill you right now,right here”
Wiliam hakutania,akamsogelea Abraham karibu na kumpiga kifuti cha pua,akamsogeza pembeni na kumtandika ngumi ya tumbo.Hakuishia hapo,akamburuza na kuanza kumshambulia ngumi zisizokuwa na idadi kamili.
“Raphael,stop”
Karishma alikuwa akipiga kelele ili Wiliam asitishe,lakini hilo halikuwezekana sababu kipondo kiliendelea.
Abraham alichakazwa,hakuweza kujitetea sababu mikono yake ilikuwa imefungwa kwa nyuma,ngumi alizopigwa hazikuwa na idadi kamili.Damu zilimvuja uso mzima,akawa hatamaniki.Hakutofautishwa na nyama buchani.Hiyo haikufanya Wiliam,mwenye hasira kama chui aliyejeruhiwa na mkuki kusitisha zoezi lake!

******


*******
ENDELEA KUSOMA HADITHI NA SIMULIZI ZA MTUNZI….EMMANUEL F.KWAY(THE STORY MASTER)

1 comment:

BLOG