Search This Blog

Sunday, May 31, 2020

SLAVE SEX SEHEMU YA 9/10


SLAVE SEX
MTUNZI….EMMANUEL F.KWAY(THE STORY MASTER)
AGE…(18+)
WatsApp…+255718 862176
SEHEMU YA 9 KATI YA 10
*******


Safari ya kwenda hospitali ikaanza,safari nzima mzee Waytte alikuwa na mawazo,hakuelewa
ingelikuwaje kama angepewa majibu ya mwanaye kipenzi kuwa ana virusi vya ukimwi,angesikitika mno sababu alikuwa ana mtoto mmoja tu na huyo ndiye alitakiwa aridhi mali zake zote.Akiwa viti vya nyuma alimuangalia mwanaye kwa huruma na kutamani kudondosha machozi.
“Baba”
“Naam mwanangu”
“Usijali nitapona”
Sebastian alimpa maneno ya kumtia moyo Baba yake hakuelewa nini kinaendelea ndani ya moyo wa baba yake, Mzee Waytte.
Dereva anayemuendeshaga Mr.Wayyte akazidi kuendesha gari mpaka walipofika hospitali ya Aghakhan, gari ikawekwa vizuri kwenye maegesho,Mr.Waytte na mwanaye wakashuka.
Jinsi Mzee Waytte alivyokuwa ana tetemeka ilikuwa ndiyo kama yeye anaenda kupima afya.
“Nisubiri hapa”
Mr.Waytee alimwambia mwanaye na kunyoosha moja kwa moja mapokezi.Haikuwa vigumu kumuhudumia sababu ni siku chache tu alikuwa ametoka hospitalini hapo,kumuuguza mwanaye Sebastian.
“Tukusaidie nini mzee?”
Msichana wa mapokezi alimuuliza Mzee Waytte kwa lugha ya kiingereza.
“Nahitaji kuonana na dokta,nina shida naye faragha”
“Alafu ndiyo sasa hivi ameingia,nyoosha tu kata kulia chumba cha kwanza”
“Sawa Ahsante”
Mzee Waytte akaanza kupiga hatua,kila alipotembea mapigo yake ya moyo yalizidi kumwenda mbio.Akafanya kama alivyoelekezwa,kabla ya kuingia akagonga mlango na kukaribishwa.
“Habari za jioni dokta”
“Salama.Ni Mr.Waytte kama sijakosea”
“Ndiyo”
“Vipi mgonjwa anaendeleaje?”
“Salama tu,sasa mimi kilichonileta hapa ni jambo moja”
“Jambo gani?”
“Nimekuja na mwanangu,nahitaji umpime virusi vya Ukimwi bila yeye kujua”
“Yaani,majibu tukupe wewe?”
“Ndiyo nachomaanisha”
“Yeye yuko wapi?”
“Yupo pale mapokezi”
“Ulimwambia unakuja naye hapa kufanya nini?”
“Nimemwambia anahitajika na daktari”
“Umefanya vizuri,nadhani upo tayari kupokea majibu ya aina yoyote yale?”
Swali hilo lilimfanya Mr.waytte amtizame Dokta Macha kwa macho yasiyokuwa na uhakika.
“Mr.Waytte”
“Naam dokta”
“Kama upo tayari,tafadhali tufanye hiyo kazi sasa hivi”
“Sawa dokta”
Mr.Waytte alisimama kutoka kitini kinyonge na kumuendea Sebastian.Baada ya dakika mbili walikuwa ofisini mwa daktari.Bado Sebastian hakuelewa ni kitu gani anapimwa na wala hakutaka kuhoji chochote kile,alikuwa nyuma ya mambo yote.Baada ya damu kubwa kuchukuliwa aliombwa atoke nje.
“Wewe nisubiri tu nje”
Mr.Waytte alisisitiza,Sebastian akatoka nje na kumuacha baba yake ndani ya chumba cha daktari.Kutokana na tekinolojia kukuwa, majibu yalikuwa tayari ndani ya dakika ishirini tu.Mzee waytte alivyomuona Daktari aliuhisi mwili wake umepigwa na ubaridi.
“Mr.Waytte”
Dokta akaita na kuvuta kiti nyuma na kukaa,akamuangalia mzee huyu machoni aliyekuwa na wasiwasi mwingi.Dokta hakutaka kupoteza wakati akatupa macho yake juu ya karatasi iliyokuwa na majibu.
“Mwanao ni HIV POSITIVE ana maambukizi ya virusi vya ukimwi na hapa tu….”
“Niniiii?”
Mzee Waytte alimkatisha daktari na kuuliza kwa simanzi, moyoni aliumia sana,ugonjwa wa Ukimwi aliuogopa kupita kiasi.Hapo ndipo mtu anayeitwa Sonia akamjia kichwani,akapata hasira zaidi alivyomkumbuka na Brenda.Huyo ndiye alikuwa chanzo cha mwanaye kupata maambukizi ya Virusi vya Ukimwi,habari hizo alipewa na rafiki yake Mr.Santiago,hakuelewa awafanye kitu gani Sonia na Brenda!

****
Sonia alijigeuza upande wa pili ili autafute usingizi,hakuwa na uhakika kama ungekuja sababu ya mawazo aliyokuwa nayo kichwani,tangu apatwe na mawaswaibu ya kutaka kuuliwa usingizi kwake ulikuwa ni kitu hadimu kupatikana,huwa anajigeuza upande wa pili lakini hakuwa analala ingawa macho huyafumba au akilala basi hatoweza kupitisha dakika thelathini bila kuzinduka,maisha yake yalikuwa ya wasiwasi kama kifaranga cha kuku sababu hakuelewa ni watu gani waliotaka kumuuwa,ndiyo maana aliwaza usiku na mchana bila kupata jibu,ingawa usoni alionesha tabasamu lililoonesha picha kuwa hana tatizo lolote lile.

Akiwa katikati ya mawazo siku hiyo usiku, alihisi ameguswa shingoni,kwa mara ya kwanza alidhani wenda yupo ndotoni lakini mkono ukazidi kumpapasa ukaanza kupita ndani ya shuka alilojifunika,hapo ndipo alipogeuza shingo yake.
“Shadrack un….”
“Shhs ssshsss”
Sonia alinyamazishwa na bastola aliyoshika Shadrack,kwa akili aliyokuwa nayo alishaelewa ni kitu gani kinachotaka kutokea mbeleni,alianza kujilaumu sana ni kwanini alimuamini mtu huyo kwa muda mfupi na kulala naye chumba kimoja.
“Tafadhali Shadrack,usifanye hivyo maa…”
“Kaa kimnya,kaa kimnya..Maana sitoshindwa kutumia nguvu”
Sonia hakutaka kuamini kuwa mwanaume aliyetokea kumuamini sasa anataka kumfanyia unyama,alizidi kuwachukia wanaume lakini alimsikitikia pia Shadrack sababu kivyovyote vile alikuwa anapakua ugonjwa wa ukimwi.
“Shadrack,usifanye ivyo tafadhali”
Sonia alijitahidi kumuokoa Shadrack lakini badala yake Shuka lake likatolewa pembeni,ndani alikuwa hajavaa kitu chochote kile,alikuwa uchi wa mnyama.Hakuwa na nguo za kubadilisha ndiyo maana usiku alikuwa akifua na asubuhi kuzivaa hizohizo.
Kitendo cha Shadrack kuuwona mwili wa Sonia ndiyo ikamchanganya zaidi,haraka akavua nguo zake na kuzitupa kando.
“Shadr..”
“Tulia lala chali,naomba usifanye zoezi likawa gumu Sonia”
Huo ndiyo mkwara aliopigwa Sonia akitishiwa bastola,katika maisha yake aliogopa kufa lakini alielewa atakufa tu.Hakuwa na jinsi zaidi ya kuanza kulia akimuurumia Shadrack ambaye alikuwa kapanda juu yake,akaishika miguu yake na kuipanua.Bila kufanya chochote akashika karoti yake na kuichomeka mgodini mwa Sonia,hakujali anamsababishia maumivu kiasi gani yeye aliendelea kumuingilia kimwili,Sonia alijitahidi kumsukumiza lakini alizidiwa nguvu,hakuweza kufanya lolote mpaka Shadrack alipomaliza mzunguko wa kwanza,tena mbaya zaidi alivunjia yai la bata ndani kwa ndani, akatulia kifuani mwa Sonia akiwa anatabasamu,lakini Sonia aliendelea kulia tu,hakuelewa ni kwanini wanaume wana tamaa kiasi hicho.

Mara ghafla mawazo ya Shadrack yakabadilika,swala la Sonia kubaki hai aliamini lingemuharibia mambo mengi sana na hakutaka swala hilo litokee, hapo ndipo alipopata wazo lingine hatari la kumuuwa kisha akamtupe baharini,hicho ndicho kitu alichokuwa anawaza kwa wakati huo.
Taratibu akajitoa kutoka kwa Sonia akavuta boxa na kuivaa.Akaitizama bastola yake,alitaka kumfyatua Sonia na risasi lakini aliogopa ingetoa mlio na ndiyo angeharibu kabisa,vitu vingi vilikuwa vinapita kichwani ni aina gani ya kifo anachostaili Sonia.
“Unaenda wapi?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Shadrack baada ya Sonia kusimama kutoka kitandani na kuvuta shuka.
“Si ushapata unachokitaka?nataka niondoke”
“Uwende wapi?”
“Kwani hapa kwetu?”
Sonia alijibu kwa hasira,kama angekuwa na nguvu angemrukia Shadrack na kumparua usoni lakini hakuwa na ubavu akabaki anaumia moyoni na kulia machozi sababu katika maisha yake hakuwahi kubakwa,maumivu ya kubakwa ndiyo ilikuwa siku ya kwanza kuyahisi siku hiyo.
“Unajibu jeuri sio?”
Shadrack akamrukia Sonia kohoni kama simba na kumlaza kitandani chali,mikono yake miwili ikawa kohoni mwa Sonia akamkandamiza ili amnyonge.Kazi ya Sonia ilikuwa ni kutupa tupa miguu yake kama kuku aliyechinjwa,Shandrack alikusudia kumuuwa kweli,alivyoona mto pembeni aliuchukua na kumfunika nao usoni.Sonia akashindwa kupata pumzi.Mpaka wakati huo alikuwa tayari anafikiria anakufa, hakuelewa ni kitu gani kinafanya mpaka watu watake kuukata uhai wake mapema,alihangaika sana kuitafuta pumzi bila mafanikio akiwa amezibwa na mto,alipapasa papasa mikono yake huku na kule akijaribu kuitoa mikono ya Shadrack iliyokuwa imekandamiza mto uliokuwa usoni mwake uliofanya ashindwe kupata hewa,alijaribu kuutetea uhai wake lakini alishindwa,hapo ndipo nguvu zikaanza kumuishia taratibu,aliamini kifo ndicho kilikuwa mbele yake.
Alinusurika mara ya kwanza porini kuuwawa kwa kupigwa risasi kisha kuchomwa moto na safari hiyo ndiyo aliamini siku zake zimefika.
“Griiii griiiii,Griii griiiii”
Mlio wa simu ulimshtua Shadrack,simu yake ilikuwa chini sakafuni, alivyopiga jicho lake chini juu ya kioo akaona jina ‘GENERAL KOMBA’ mkuu wake wa kazi,hakuelewa ni kwanini anampigia usiku huo,alitamani kuipokea lakini ilibidi amalize zoezi alilolianza,simu ilikatika na ikaita tena.
Hapo ndipo alipoachana na Sonia na kuinama kidogo akaichukuwa simu na kuipokea.
“Naam mkuu”
“Upo wapi?”
“Mimi,mimi nipo hapa Hotelini mkuu”
“Upo na yule binti bado?”
Lilikuwa ni swali lililom-babaisha Shadrack,alivyomuangalia Sonia alikuwa ametulia tuli.Mapigo yake ya moyo yakaanza kumpiga kwa nguvu,akashindwa kutoa jibu la moja kwa moja, ndiyo maana akabaki kimnya.
“Upo na yule binti,mbona hujibu?”
“Hapana”
“Upo chumba namba ngapi?nipo nje ya hotel nahitaji kuonana nawewe”
“Mimi,mimi Subiri kidogo nimesahau chumba namba ngapi Mkuu”
“Nataka kuja hapo,fanya uniambie”
“Sawa Mkuu”
Shadrack alihisi kuchanganyikiwa akakata simu,Sonia alikuwa ametulia tayari,zoezi alilofanya lilikuwa limekamilika la kumuuwa.
Kabla ya kufanya kitu chochote simu yake ikaita tena jina likatokea lile lile ‘General Komba’akazidi kuhaha,akaichukuwa na kuipokea.
“Naam mkuu”
“Upo chumba namba 102 nakuja,nimeuliza hapa mapokezi”
“Mkuu,naam sawa sawa”
Kijasho kilimtoka Shadrack akashindwa kuelewa ni kitu gani akifanye,alivyoangalia kushoto kwake akaona mlango wa bafuni,akamvuta Sonia kutoka kitandani na kumburuza mpaka bafuni,akamlaza hukohuko ili baadaye akamtupe.Akaweka kila kitu sawa,na kujifuta majasho.
“Ngo ngo ngo ngo”
Mlango uligongwa!Shadrack akatembea kwa kunyata huku akiangalia kama kila kitu kipo sawa,akachukuwa bastola yake iliyokuwa kitandani na kuichomeka kiunoni.Alivyofungua mlango akapiga saluti na kuchapa mguu chini kumaanisha kuwa aliyeingia ni mkubwa wake wa kazi.
“Karibu mkuu”
“Ulisema yule binti hayupo?”
Lilikuwa ni swali la kwanza kutoka kwa General Komba tena bila kujibu salamu.
“Ndio mkuu hayupo”
“Mbona nilivyoulizia mapokezi nikaambiwa hakutoka na hajawahi kutoka huku ndani?”
“Alitoka leo jioni saa kumi,nadhani aliyekwambia hakuwepo yeye.Atakuwa ameingia mwingine shifti”
“Okay sawa.Tutaondoka wote sasa hivi tunaenda kwa Captain Mustapha”
“Lakini mkuu,kule si yup…”
“Tangu lini umeanza kupinga kauli zangu?”
Sura ya General Komba ilikuwa ya kutisha na aliogopeka mno,katika uongozi wake alichukia kubishiwa kauli,hata kama angekwambia utoe haja kubwa mbele ya kadamnasi, alitaka utii amri.
“Samahani mkuu”
“Sawa,tutaongozana kwa sababu wote hawapo Hospitalini na kitu kilichonileta hapa ninataka maelezo yako,ilikuwaje?”
“Siku hiyo ilikuwa Madale tupo nda…”
“Utakuwa unanielezea huku tunaenda”
“Sawa mkuu”
Kichwa cha Shadrack kilikuwa waluwalu kimevurugika,hakuelewa ni kitu gani akifanye aliuangalia mlango wa bafuni mara mbili mbili huku akitoka nje, General Komba akiwa mbele yake.

*****

Alichohisi ni maumivu shingoni makali,bado kumbukumbu zake zilishindwa kukaa sawa.Taratibu alifumbua macho yake na kujikuta yupo uchi wa mnyama bafuni,hapo ndipo alipokumbuka kuwa alihitajika kuuwawa na Shadrack baada ya kubakwa,bado hakuamini kuwa yupo hai au amekufa.Alitembea taratibu na kusikilizia kama kuna mtu yoyote yule,alifungua mlango wa bafuni na kukitizama chumba, hakukuwa na dalili ya mtu yoyote yule,hakuelewa ni kitu gani akifanye lakini akili yake ilimwambia kuwa atoke mara moja na kukimbia.
***
“Mkuu samahani kidogo,kuna kitu nimesahau chumbani”
Shadrack alisema baada ya kufika ndani ya gari na General Komba,bado hakuwa na imani kama Sonia alikufa kweli.
“Kitu gani hiko?fanya haraka basi”
“Sawa”
Shadrack alishuka ndani ya gari na kuingia haraka hotelini,alikuwa anamuwahi Sonia,akahakikishe ni kweli alikuwa amekufa machale yalimcheza,jinsi alivyopanda ngazi ilitisha,aliruka ngazi tatu tatu.Sonia aliyekuwa chumbani alihisi kishindo cha mtu tena kinakuja usawa wa chumba alichokuwepo,kupitia kitasa cha mlangoni alimuona Shadrack akikoki bastola yake anataka kuingia chumba alichokuwepo,hapo ndipo alijua kuwa ndiyo mwisho wake,hakuwa na ujanja wowote ule.Wazo lililomjia ni kurudi bafuni haraka,hicho ndicho alichokifanya bahati kwake alikuwa bado hajaweka nguo mwilini,akaingia bafuni na kujifungia kwa ndani.
Shadrack akazama ndani moja kwa moja akaufikia mlango wa bafuni na kunyonga kitasa.Kilichomchanganya akili yake mlango haukufunguka,akalazimisha lakini wapi!
Kwa nguvu zake zote alirudi nyuma na kuupiga kwa nguvu mlango,akauvunja na kuingia bafuni.


 Sijui akili hiyo aliitoa wapi ya kulala sakafuni kama alivyojikuta mara ya kwanza amezirai,hakuelewa kama kitu anachokifanya kilikuwa sahihi kujiokoa na muuaji Shadrack ambaye alikuwa anahangaika kuufungua mlango aingie ndani ampige risasi.Sonia alilala sakafuni akiwa hivyohivyo uchi wa mnyama bila kujitingisha,mapigo yake ya moyo yalidunda kwa nguvu.Alisikia mlango wa bafuni umevunjwa na Shadrack kuingia ndani.Kitendo cha Shadrack kukuta mlango umefungwa kilimchanganya akili yake hakuelewa umefungwa vipi lakini alivyoingia bafuni alishindwa kupata jibu sahihi baada ya kumkuta Sonia bado amelala kama alivyomuacha.
“Itakuwa niliufunga”
Shadrack aliwaza lakini bado hakuamini kwamba Sonia alikufa,ilikuwa ni lazima ahakikishe hapo ndipo alipotembea mpaka alipo.
“Griii griiiii”
Simu iliyokuwa mfukoni mwake ndiyo ilimshtua akasitisha zoezi la kuinama ili kuhakikisha uhai wa Sonia.
“Fanya haraka Shadrack”
Upande wa pili wa simu ulimsisitiza ukitokea kwa General Komba aliyekuwa nje anamsubiri.
Shadrack akasita kidogo,akaingalia bastola yake na kumtizama Sonia aliyekuwa chini,akarudi mpaka chumbani na kuchukuwa shuka,akaliviringisha mbele ya bastola ili isitoe mlio atakapoifyatua.
Akarudi nayo bafuni na kuikoki,akamuelekezea Sonia usawa wa kichwani.Bado alijisikia kumuuwa Sonia lakini upande mwingine wa pili ulimwambia akifanya ivyo ndiyo ataharibu,akaghairi na kuinama kidogo.Akaweka mkono wake mmoja puani kwa Sonia ili kusikiliza Pumzi.Akatulia kwa kama sekunde mbili nzima mkono wake ukiwa chini ya pua za Sonia,hewa ilikuwa haitoki hiyo ilimaanisha mapigo ya Moyo wa Sonia yameacha kupiga,amekufa tayari.
Akashusha pumzi na kutoka harakaharaka baada ya simu yake kuita,General Komba ndiyo alikuwa akipiga kwa mara nyingine,kutokana na hofu ilibidi atoke chumbani,akafunga mlango wa kuingilia na funguo kisha akaziweka mfukoni.

Sonia alikurupuka na kukohoa baada ya kuzibana pumzi zake kwa kama dakika mbili nzima alivyohisi Shedrack ameondoka,alihema harakaharaka kama mtu aliyetoka kukimbika umbali wa mita nyingi,hakuamini kama amepona sababu alijihesabia ni maiti mtarajiwa,hapohapo akasimama mpaka dirishani akachungulia kwenye kioo na kumuona Shadrack anaingia ndani ya gari la Jeshi.
Bila kuchelewa alivaa nguo zake harakaharaka,na kuukimbilia mlango.Moyo wake ukapiga kwa nguvu alivyogundua mlango umefungwa na funguo,alikuwa ana uhakika kuwa Shadrack angerudi na kummaliza endapo angemkuta chumbani,ilibidi afikirie jinsi ya kutoka ndani ya chumba kabla ya Shadrack kurejea!
***
Hali ya Captain Mustapha haikuwa ya kuridhisha,risasi aliyopigwa ilichimba na kutoboa mfupa wake mguuni.Hali yake ikafanya madaktari wasukume machela mpaka kitengo maalumu cha mifupa,wakaonana na Dokta Lukubilo.
“Mpelekeni thieta haraka sana”
Daktari huyo ambaye alibobea na kucheza na mifupa ya binadamu wenzake alitoa agizo hilo na ndiyo huyo aliyekuwa daktari wa kiafrika,wenzake wote walikuwa wahindi.
Walimuamini kupita kiasi,hakuna mfupa wowote wa binadamu ungeshindwa kuchambuliwa na Mwanamama Lukubilo.Kila alipokwenda Nasra alikuwa nyumanyuma kama mkia,alilia machozi,Mchumba wake Mustapha alikuwa katika hali mbaya sana.Hakutaka kusikia habari kuwa atakuwa anatembelea kiti cha matairi katika maisha yake yote.
“Dokta tafadhaliii,Musta..pha mpenzi”
Nasra alikuwa akilia na kuifata machela iliyozungukwa na jopo la madaktari saba, akiwepo Dokta Lukubilo.
“Dada tafadhali,subiri hapo”
“Ni mchumba wangu”
“Na sisi ni mgonjwa wetu”
Nasra alisubiri juu ya benchi huku akilia machozi,Mustapha alikuwa kila kitu katika maisha yake,ndiyo maana alijisikia uchungu ajabu!
Kitanda chake kikaingizwa chumba cha operesheni ili waitoe risasi kwa uangalifu iliyozama ndani ya mfupa,ulihitajika umakini wa hali ya juu ili isisababishe maafa.Ndiyo maana Dokta Lukubilo akaingilia zoezi hilo kati.
“Ganzi bado haijakolea,weka cc 12 haraka sana”
Dokta Lukubilo alisema wakiwa ndani ya chumba cha upasuaji,kila alichoagiza kilifanyika dakika hiyo hiyo.
***
Haikuwa kazi rahisi kukituliza kilio cha Nasra,wanajeshi walim-bembeleza bila mafanikio wakiwa tayari wamefika,hata wao walikuwa na usongo na watu waliomjeruhi mwenzao ndiyo maana baadhi ya wanajeshi walirudi msitu wa Madale kufuatilia.
M.P Magdalena John alikuwa bega kwa bega na Nasra.
“Nasra pole,Mustapha atapona risasi haijamjeruhi sana”
“Ahs..nte”
Nasra aliendelea kulia tu.Mpaka dakika ishirini zinapita chumba cha operesheni bado kilikuwa ‘bize’hakuonekana daktari yoyote kutoka,Nasra alikuwa ana kihoro cha kutaka kujua kilichoendelea ndiyo maana macho yake yalikuwa mlangoni.
Bado aliendelea kububujikwa na machozi yakalowanisha nguo yake ya juu,akimlilia mchumba wake Mustapha aliyekuwa chumba cha upasuaji.
Ghafla akaona mlango unafunguliwa,akasimama na kumuendea Dokta kwa haraka.
“Vipi hali ya mchumba wangu?”
“Sio mbaya,tumeitoa risasi”
“Atapona?”
Lilikuwa ni swali lingine kutoka kwa Nasra.
“Tumuachie Mungu,sisi tushafanya kazi yetu”
Dokta Lukubilo akamaliza na kutembea akielekea ofisini kwake,hazikupita hata sekunde tatu machela aliyolala Mustapha ikatolewa huku akiwa amefungwa bandeji mguuni.Bado alikuwa hana fahamu.Nasra akabaki kuitizama machela,mpaka ikiingizwa ndani ya chumba kingine ambapo hakuruhusiwa kuingia kwa wakati huo.
***
Kuanzia siku hiyo hali ya Mustapha iliendelea kuwa nzuri kadri siku zilivyozidi kwenda mbele,aliweza kutembea wodini akifanya mazoezi akiwa na mpenzi wake Nasra,kila siku alifanya mazoezi ya kutembea akitumia magongo pembeni akiwa na mpenzi wake.Alijihisi kupona na alifarijika sana,hiyo ndiyo ilimfanya apone harakaharaka.
“Baby,embu tembea acha magongo utadumaa”
“Najitahidi hapa mpenzi”
“Kila siku unajitahidi tu”
“Ndio,mguu bado unauma”
“Unanipenda?”
“Kuliko unavyodhani”
“Nipatie hayo magongo”
“Sasa nitatembeaje lakini?”
“wewe nipatie”
“Baby”
“Please”
Yalikuwa ni maongezi ya mtu na mpenzi wake siku hiyo wodini,Nasra alijaribu kila analoweza ili Mustapha apone haraka.Ndiyo maana hata aliomba ruksa kazini kwa muda wa siku saba ili amuuguze Mpenzi wake hospitalini.
“Ayo hapo”
Nasra akakabidhiwa magongo,akatembea nayo na kukaa kitanda cha pili.
“Nifuate hapa,jitahidi mpenzi”
Mustapha alijitahidi kutumia nguvu kutoka kitandani alipo bila msaada wa magongo,alisimama kwa tabu na kupiga hatua ya kwanza,alivyopiga ya pili alishindwa na kuporomoka mpaka chini mzima mzima,bado alikuwa anaumwa.Nesi aliyekuwa pembeni aligeuka,kishindo kilimshtua.
“Ndiyo nini sasa?”
Nesi alifoka kwa sauti ya hasira,kitendo hicho kilimkera sana.
“Mgonjwa bado hajapona,unataka kuleta tena majanga”
Nesi alimfokea Nasra kwa kitendo cha kujaribu zoezi lake.
“Sisi sio wajinga kumpa magongo,embu toka kwanza”
Damu zilivuja nyingi zikitokea kwenye jeraha la Mustapha,alijitonesha kidonda chake.Nasra alichanganyikiwa na kutoka nje akijutia kwa kitendo alichokifanya.Ulikuwa usiku mnene na alilazimika kulala Hospitali kila siku.
“Excuse me!”
Ilikuwa ni sauti iliyomtoa Nasra katika mawazo,akainua kichwa chake juu akijaribu kumtizama mwanaume aliyemgusa begani.
“Do i know you?”(Sijui,tunafahamiana)
Sebastian ndiye alikuwa mbele ya Nasra kamshika begani,sura ya mwanamke huyo haikuwa ngeni machoni mwake ingawa hakuelewa ni wapi alikutana naye.
“I’m not so sure but i think we met somewhere”(Sina uhakika lakini nadhani,tulishawahi onana mahali)
Nasra alijibu huku akijifuta machozi akitumia viganja vyake vya mikononi.Wa kwanza kupata kumbukumbu alikuwa ni Sebastian akamkumbusha alivyomsaidia kwenye duka la nguo alivyotaka kupigwa akisingiziwa kuwa ni mwizi,hapo ndipo wakapeana mikono.
“What are you doing here my friend? I thought you have left already”(Nini unafanya hapa,nilidhani ulishaondoka tayari)
“I had some zibs but now I’m okay I’m cool.So what’s up?”(Nilikuwa na matatizo lakini sasa hivi niko poa)
Sebastian kama kawaida yake,aliongea kiingereza chenye ‘swagga’ huku akiupindisha mdomo wake kwa mikogo kama msanii,aliongea kwa mapozi yaliyopitiliza.Kabla ya maongezi yao kufika mbali ghafla wakatokeza watu wawili,mmoja tu ndiye Nasra alimtambua,Shadrack.
“Mkuu,binti mwenyewe ndio huyu hapa”
Shadrack alitokeza na General Komba,wakapeana mikono na kumsalimia Sebastian.
Bado akili ya Shadrack ilikuwa kwa Sonia na ilikuwa ni lazima arudi hotelini kabla ya asubuhi kukucha,ndiyo maana alimfikisha General Komba hospitali na kuongea kila kilichotokea harakaharaka.
“Sawa unaweza kuendelea na shughuli zako Shadrack,nitabaki na huyu binti hapa anisimulie kilichotokea”
“Sawa mkuu”
General Komba hakuelewa kuwa anaruhusu umauti wa Sonia.
Ruksa kutoka kwa General ndiyo kitu alichokuwa anakiomba Kwa Mungu kitokee,mwili wa Sonia kukutwa hotelini kingemaanisha kuwa mahali pabaya,haraka akaanza kukimbia kutoka nje.Akakodi Taxi huku akimsisitiza dereva afanye awezalo ili afike mapema!
****
Sonia alitafuta kila njia ili aokoe uhai wake,alipiga piga mlango bila kupata msaada wowote ule,alicheza na kitasa bila kuambulia kitu chochote alivyoangalia pembeni aliona simu ya mezani,hapo ndipo moyo wake ukatulia ilikuwa ni lazima apige simu mapokezi kuomba msaada,alivyoinua mkonga hakusikia chochote.Alihisi kuchoka baada ya kuona nyaya za simu zimekatwa lakini hakukata tamaa hata kidogo alizidi kutafakari ni kitu gani akifanye,mara ghafla akahisi kishindo cha mtu kinapandisha ngazi.Hapo ndipo aliona mwisho wake unafika,kilichomchanganya zaidi alihisi mlango wake unataka kufunguliwa,hakuelewa ni kitu gani akifanye.
“Ngo ngo ngo”
Mlango uligongwa kwa muda mrefu.
“Na na nana nani?”
“Muhudumu”
Sonia alivyosikia hivyo,moyo wake ukapiga mkambo akasogea mpaka mlangoni.
“Dada kuna funguo za ziada unifungulie?”
“Kwani huna funguo?”
Badala ya kujibu swali muhudumu akauliza swali,likawa swali juu ya swali.
“Sina,tafadhali naomba nifungulie mlango”
“Sawa,nakuja ngoja nikaangalie funguo za spea”
Ilikuwa ni asante Mungu kwake.Alifurahi kupata uhuru,baada ya muda kidogo akahisi ufunguo umeingia ndani ya kitasa chake.Akatabasamu lakini ulivyofunguliwa mapigo yake ya moyo yakapiga paa!
Alikuwa ni Shadrack ameingia.
“Kumbe upo hai?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Shadrack,akiwa haamini hata yeye.Sonia alirudi kinyumenyume kwa uwoga.
“Dada,eeh samahani”
Muhudumu wa Hotelini ndiye aliingia ghafla lakini aliomba radhi baada ya kumkuta Sonia yupo na mwanaume.
“Muhudumu”
Sonia akaita.
“Kuna tatizo?”
“Naomba nikwambie kitu,njoo mara moja”
“Hapana dada nyie endeleeni tu”
“Hapana tafadhali”
“Dada asikusumbue,endelea na mambo yako”
Shadrack akatoa kauli na kumgeukia muhudumu hapo ndipo Sonia alipompiga kikumbo cha nguvu Shadrack na kutoka mlangoni kama kichaa,jinsi alivyoshuka ngazi iliogopesha,alikimbia kama hana akili nzuri.
Haraka akatoka nje akapita mapokezi huku akikimbia.Mpaka kutoka nje.
“Boda boda”
Alivyoita tu,pikipiki ikafika miguuni mwake.
“Nipeleke Mikocheni B”
“Sawa twende”
Kitendo cha kupakia nyuma,pikipiki ikatimua mbio.Alivyogeuka nyuma alimuona Shadrack katokeza hotelini.
“Kaka nawahi jaribu kuongeza mwendo”
Dereva akatii amri ya mteja wake,akazidi kubadili gia.
Mpaka anafika nyumbani kwake usiku huo hakuamini amepona na yupo hai anapumua,alinusurika kifo mara mbili mfululizo.
“Kaka nisubiri hapa nakuja sasa hivi”
“Sawa usichelewe basi”
“Dakika moja”
Sonia akaingia ndani kwake na kukuta vitu kama vilivyo,simu yake juu ya kochi.Hakutaka kupoteza wakati akaingia chumbani kwake na kutoka na noti ya shilingi elfu kumi,alivyotoka nje ya geti alimkuta dereva akimsubiri.
“Kaka samahani”
“Bila samahani dada angu,sasa hapa chenji sina sijui itakuwaje”
“Usijali kaka angu,lakini naomba kitu kimoja”
“Kitu gani?”
“Usimuoneshe mtu yoyote yule hapa kwangu”
“Hilo usijali”
“sawa usiku mwema”
Sonia alirudi ndani,alivyoangalia simu yake ilikuwa imezima haina chaji,alichofanya ni kuiweka kwenye umeme ili ijae aangalie utaratibu mwingine.
Aliogopa kukaa mwenyewe ndani ya nyumba yake.
“Hapa silali leo”
Aljisemea mwenyewe huku akitafuta funguo zake za gari lakini kabla ya kuzipata alihisi geti lake linagongwa kwa fujo,hapo ndipo alipochanganyikiwa.Alishindwa kuelewa ni kitu gani akifanye akabaki njia panda.
“Weweeeee mwanamkeeeeee,funguaaa malaayaaa weweeeeeee,Wewe kaluma Kengeee”
Ilikuwa ni sauti ya kilevi,kilichomkera ni geti lake lilivyokuwa linagongwa.Akatoka nje taratibu na kufungua geti kwa taadhari.
“Mamaaa Kibakuuuliii,eeeeh jamaaani kuumbee nimepoteeaaaa,any way kumbe sio kwangu hapaaaa…so sorry my dear neighbour”
Mlevi aliongea akipepesuka,Sonia alisonya na kufunga geti.


****
Mchezo wa Leythan ulikuwa ni uleule tu,alibadilisha wanawake kama nguo,leo huyu kesho yule.Kwa jinsi alivyokuwa mzuri na mwenye mwili wa mazoezi hata angekuwa nani asingeweza kumchomolea hiyo ikamfanya azidi kuwachanganya wanawake kama pilau na kachumbari.Leythan alipenda vimwana,mtaa aliokuwa anaishi alishatembea na wake za watu karibia wote.
Na haikuwa rahisi kwa Leythan kukutana na mwanamke kingono kesho yake asirudi.Alijua kucheza na mwili wa mwanamke awe mnene au mwembamba wote aliwajulia, Leythan alipenda ngono.Lakini mbali na yote hayo alifanya mambo hayo kwa siri kubwa mno,Conie ndiye alimuweka mjini kila kitu kuanzia nguo mpaka malazi ilikuwa ni juu ya Conie.
Walijificha Mombasa kwa takribani Miezi mitatu bila kugundulika.
“Shika hii mpenzi”
“Ya nini?”
“Basi tu,utaweka vocha simu yako”
“Ahsante”
Ilikuwa ni pesa kama pongezi kutoka kwa Mwanamke aliyeitwa Linnah,na ilikuwa ndiyo siku yao ya kwanza kukutana wakakodi hotel kubwa katikati ya mji wa Mombasa,Linnah hakuelewa lolote kuwa anachukuwa maambukizi ya ukimwi kutoka kwa Leythan.
Kitendo cha kufanya ngono na kufikishwa mshindo kilimchanganya akili yake jumlajumla ndiyo maana akatoa hongo ya shilingi elfu mbili za Kenya.Kwa Leythan alitabasamu na kuelewa kuwa kibarua alichokifanya hakikuwa cha kawaida.
“Ibra”
“Naam”
“Una Mke?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Linnah,akiwa kifuani kwa Leythan anamkwaruza na kucha zake zilizokuwa fupifupi kiasi.Jina la Ibrahim ndilo alikuwa analitumia ili asigundulike.
“Mh,ninae ndiyo”
“Mbona hauna pete ya Ndoa?”
“Sorry,nina girlfriend tu.Swali lako sikulielewa vizuri.Kule bongo sisi tumezoea Mke ndiyo huyo huyo mchumba awe demu wako sisi tunasema mke”
“Lakini hauna mmoja?”
“Ndio,ninaye yeye nawewe.Ninao wawili”
“Sio hivyo,ukinitoa mimi”
“Hapana sina mwingine”
“Kweli?”
“Haki ya Mungu tena”
Maongezi yaliendelea chumbani kimahaba,mkono wa Linnah ukapita taratibu na kuanza kushikashika gobole la Leythan lililokuwa limeanza kuvimba kiasi,akaanza kulichuwa.Bado Linnah hakukata kiu yake sawa sawia na ndiyo maana alitaka tendo upya,taratibu jogoo wa Leythan akaanza kusimama na mwishowe kukaa wima kama msumari.Hicho ndicho kitu alichokuwa anasubiri Linnah muda mrefu.
Alivyotaka kumpiga denda Leythan, alitulizwa.
“Baby si tukaoge kwanza”
“Baby bwaana aaaah!”
Linnah akaongea kwa sauti ya puani,ilikuwa ni kama amekatwa stimu.Mwili wake ulikuwa unachemka kama maji ndani ya hita.
“Tukaoge,tuwe wasafi”
“Ahh!”
Linnah alionesha kukasirika lakini hakuwa na jinsi wote wakasimama, Leythan akiwa nyuma yake kamshika kiuno wapo uchi wa mnyama mpaka bafuni.Uzuri wa chumba hicho kilikuwa ‘self contained’ yaani choo na bafu vipo ndani kwa ndani.
Wakiwa wamekumbatiana hivyohivyo walisogea mpaka kwenye koki ya bomba la mvua na kulifungua.Maji yalipoanza kuwamwagikia,Leythan aliuvuta mdomo wa Linnah akatoa ulimi wake nje akautumbukiza mdomoni mwa Linnah wakaanza kunyonyana ndimi,ngoma haikushia hapo!
Mkono wa Leythan ulianza kupapasa maziwa ya Linnah juu ya chuchu zake,hakuishia hapo akashuka mpaka njia ya kwenda ikulu akakumbana na kinyama kidogo mithili ya kiharage.Hicho ndicho alichoanza kucheza nacho taratibu mno,mara akifikiche mara akipapase.Hiyo ilimchanganya zaidi Linnah aliyeanza kuguna ndani kwa ndani huku akizidisha kasi ya kuunyonya ulimi wa Leythan uliokuwa ndani ya mdomo wake,raha alizohisi zilizidi kipimo chake ndiyo maana akaanza kushika shika koki za mabomba,hakuelewa ni kitu gani akifanye kwa wakati huo.
Alihisi yupo angani vitu vyote anaviona kwa chini.Leythan alishalielewa hilo,akazidi kucheza na kinyama hiko kilichokuwa mkabala na ikulu,akatumia kidole kimoja kukipenyeza ndani ya ikulu ambayo ilikuwa na hali joto ya sentigredi kumi na tisa.Akaanza kupima oil,kwa jinsi alivyochezesha kidole chake ndani ya ikulu hakutofautishwa na mtu anayekikuna kipele.
Leythan alikuwa hodari wa ngono,na alielewa hiyo ndiyo ingempagawisha Linnah zaidi.Mambo hayakuishia hapo,aliuchukuwa mguu mmoja wa Linnah na kuupandisha juu kidogo,akainamisha kichwa chake na kutoa ulimi wake,akaugusisha juu ya kinyama kilaini na kuanza kukinyonya akafanya kama anamung’unya ubuyu.Mambo yalikuwa mukidemukide,mpaka hapo Ikulu ya Linnah ilishatengeneza uteute ikawa imelowa tayari ingawa kulikuwa na maji yanamiminika kutokea juu ya bomba lakini Leythan alilijua hilo.Akapitisha ulimi wake ndani ya ikulu na kuanza kudeki bahari.
“Ahh mmh aaaah Ibraaaaaa,aaaaaah aaaahh”
Hapo ndipo Linnah alipokuwa hajiwezi tena alihisi kufakufa,raha zilizidi kipimo.Ulikuwa ni ufundi wa hali ya juu na uliokwenda shule.Kufumba na kufumbua hakuelewa ni wakati gani ndizi ya Leythan imeingia ndani ya mgodi wake.Akabebwa kama mtoto mpaka chumbani akatupwa kitandani Puu! Hapo hapo Leythan alipanda juu yake,akaseti mitambo na kumchomeka nyoka wake mrefu na mnene kiasi ndani ya mgodi huo wenye hali ya ujoto.
****

Afande Maria pamoja na askari mwenzake aliyefahamika kwa jina la Simon Peter kidoletumbo,waliingia Mombasa saa tano za usiku na basi la kampuni ya Modern Coast ambalo liliwatoa katikati ya jiji la Nairobi.
Ilikuwa ni safari ndefu iliyowachosha viungo vyote vya mwili.Siku mbili mfululizo wakitokea nchini Tanzania jijini Dar es salaam.Kazi iliyowapeleka jijini humo ni kumtia mkononi Leythan Jabir kisha awatajie ni wapi Conie alipo,haikuwa kazi ngumu kufika eneo lililoitwa Nyali,lilikuwa ni eneo lililochangamka,eneo hilo ndilo waliambiwa Leythan anapatikana.

Kutokana na uzoefu wao wa kazi swala la kumkamata Leythan lilikuwa ni sawa na kuweka kibakuli cha supu mdomoni!
Walivyoshuka tu walitafuta hotel ili kesho yake waanze msako wao kimnya kimnya.
“Sasa afande,wacha nikutakie usiku mwema.Maana nilivyochoka Mungu anajua.Khaa!”
Afande Maria alimwambia Mwezake huku akiwa katika hali ya uchovu.Ndani ya hotel hiyo kila mtu alipewa chumba chake cha kulala.
“Hata mimi aise,viungo vyote vinauma”
“Basi poa,kesho”
“Aya usiku mwema”
Waliagana na kila mtu akachukuwa chumba chake.Katika jeshi la polisi na swala la upelelezi walimtegemea sana Afande Maria,linapokuja swala la kufuatilia kesi hakutaka mchezo.Ungepewa picha yake na ungeambiwa kuwa ana roho mbaya ungebisha.Maria alikuwa mzuri wa sura,macho yake madogo yaliendana na mashavu yake manene kiasi.Alikuwa ana mdomo mdogo wenye ‘lips’ nyembamba sana.Pua yake ilijichonga vizuri kama za watu wa Rwanda.
Afande Maria alibarikiwa kupewa umbo kubwa kushuka chini ya kiuno,hips zake zilisambaa pembeni na kumfanya ajichonge vizuri.Maaskari wenzake siku zote walikuwa wakimuita ‘bata mzinga’ kutokana na umbo lake.
Ni askari huyo tu ndiye hakuwa na huruma hata siku moja,alishawahi kumtishia bosi wake bastola na ilikuwa kidogo amuulie mbali,Maria hakumuogopa mtu yoyote yule.Alimpania Leythan kupita kiasi,alikuwa ana usongo wa kumtia mikononi mwake.Ndiyo maana alivyofika tu alichukuwa picha ya Leythan na kuitizama vizuri akasimama na kufungua pazia,akaangalia kwa chini jinsi watu wanavyotembea tembea.
“Kesho nitaanza kwenye ule mgahawa,inabidi nijenge urafiki kwanza na watu wawili watatu”
Afande Maria aliwaza,akaingia bafuni kujimwagia maji na kujitupa kitandani,kutokana na uchovu usingizi ulimzoa hapohapo!
***
Jiji la Mombasa lilikuwa dogo mchana lakini usiku lina mambo mazito tena ya kikubwa,mbali na hapo lilisifika kuwa na ‘mabahasha’haukutofautishwa na sodoma na gomola usiku.Wasichana wazuri walijiuza waziwazi na wanaume pia walifanya ushoga kupindukia!Club iliyoitwa Tembo siku hiyo ilikuwa kufuru.
Watu walishona ndani ya club hiyo,madada poa walikuwepo.
Mapema saa mbili kulikuwa na burudani ya wanawake waliovalia mavazi ya kihindi wanacheza.Hapo ndipo Afande Maria alipoamua kufika na kuangalia mazingira akipoteza muda.
“Heheheheiyaaaaaa!Weka mambo,weka mambo.Nipe rahaaaa mieeeee”
Wanawake walikuwa wakinyonga viuno vyao na baadhi yao wakianza kuvua nguo moja baada ya nyingine.Wanaojua kutumia pesa walizitumbua.
“Mimi ndiyo sonkooooo wa Kenya nzimaaaaa,nataka kiuno cha elfu kumi mwaga mauno,mwaga mauno Mama,nataka cha elfu kumi”
Sauti hiyo ilitokea kwenye kipaza sauti,mwanaume aliyeshika kipaza sauti alipagawishwa na viuno vya wanawake kazi yake ilikuwa ni kumwaga pesa. Kwake ilikuwa burudani watu walishangilia.
Hilo ndilo lilikuwa jii la raha,Mombasa.

Ilivyogonga saa saba mmoja baada ya mmoja alianza kusambaa wakabaki watu wachache.Afande Maria alivyotaka kusimama na kuondoka akasita baada ya kuona kikundi cha watu kimeingia,walianza wanaume wenye miili mikubwa kisha katikati yao alikuwa kijana mdogo aliyevalia suti nyeupe.Kwa harakaharaka alionekana ni mwenye pesa au Sonko kama walivyozoea kusema kwa lugha yao.
“Dada mambo”
Sauti hiyo ilimshtua Afande Maria,akageuka.
“Poa”
“Samahani kidogo,chif Olongo ameingia kwahiyo naomba utupishe hapa.Ukakae kule”
“Sasa si nimelipia kukaa hapa?”
“Ndio naelewa lakini nakuomba”
Afande Maria hakutaka shali,akasimama na kinywaji chake mpaka kaunta na kukaa.
Ni kweli Mtu wa katikati kavaa suti nyeupe alikuwa ni Chif Olongo,alikuwa ni miongoni mwa matajiri wenye umri mdogo.Ilikuwa ni lazima aache stori nyuma endapo akiingia club yoyote ile.Pembeni kushoto alikuwa na mwanamke mweupe mnyasa,mrefu futi kadhaa kwenda hewani,alikuwa ni mwanamke mzuri mwembaba,huyu ndiye alikuwa hawala wa Chif Olongo.
“Baby naenda kucheza kaunta ya juu”
“Poa”
Hawala wa Chif Olongo aliogopeka kupita kiasi,muda wote alitembea na walinzi,Chif Olongo alimlinda kama mtoto wa Mfalme aliapa kula sahani moja na mwanaume yoyote yule atakaye kuwa naye karibu.
Ni kweli alipanda gorofa ya juu kwenda kucheza mziki,alivyoingia katikati hakuna hata mwanaume mmoja aliyemsogelea.Watu walimuogopa Chif Olongo.
“Mh,mbona mtoto mzuri hivyo.Hana mtu au?”
Leythan alijiuliza maswali mengi akiwa kona ya mwisho pembeni yake kulia ameketi na Conie,wanakunywa bia.Alimuangalia mwanamke mrefu mwembamba akiwa anacheza peke yake katikati.Udenda ukamtoka.
“Baby, mbona unamuangalia sana yule demu?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Conie.
“Kwani vibaya love?anacheza vizuri”
“Unataka kwenda kucheza naye?”
“Ukiniruhusu poa tu”
“Nyooo nani kasema,embu tulizana hapo bwana mdogo”
“Ha! Haa! Haaa! Haaaaa! Haaaa!”
Wote walicheka,lakini Leythan alimuangalia kwa jicho la matamanio,hapohapo alimvua nguo kihisia akamchungulia ndani.Akampeleka kitandani,ni kweli alimuhitaji lakini hakuelewa ni kwa namna gani angeweza kumpata,akili yake bado ilikuwa inafanya kazi bila kupata jibu la harakaharaka.Ilikuwa ni kama Mungu akamuona anaelekea gizani upande wa chooni.Nayeye akasogeza kiti nyuma na kusimama.
“Baby nakuja”
“Unaenda wapi?”
“Chooni,mkojo umenibana”
“Malizia basi hii bia,niagize nyingine”
Ili kutoa usumbufu Leythan akachukuwa glasi iliyokuwa na bia nusu akainywa yote kwa mkupuo na kuanza kutembea kuelekea chooni.
Katika maisha yake hakumuogopa mwanamke hata siku moja,alikuwa ni mwanaume jasiri.Hata angekuwa mtoto wa Raisi Leythan angemfuata tu.
Bila kujali akaingia choo cha wanawake.
“Mambo”
Leythan alisalimia baada ya kumuona mwanamke huyo mrefu katoka kutoa haja ndogo!
“Safi”
Alijibiwa kifupi na kupitwa kando,kabla ya mrembo huyo kufika mbali alimshika mkono na kumzuia asitoke nje.
“Mbona hivyo mrembo?”
“Hivyo vipi?Embu niachie”
“Nisikilize kwanza ndiyo nikuachie”
“Wewe kaka vipi?”
“Mimi naitwa Ibrahim”
“Ahsante kwa kukufahamu”
Leythan alipandishwa juu mpaka chini,na macho ya mwanadada huyo.Na kutaka kuondoka lakini Leythan alizidi kumzuia.
“Sasa utaondokaje bila kunitajia jina lako?”
“Kwani lazima?ujue nitapiga kelele”
“Wala siogopi wewe piga tu”
“Niache basi niende,usijitafutie matatizo”
“Wacha nipate kwa ajili yako”
“Unataka nini?”
“Kujua jina lako”
“Naitwa Jemima,aya niachie”
“Uko peke yako?”
“Nipo na mume wangu”
“Sawa,upo mpaka saa ngapi?”
“Kaka niachie basi”
Jemima akatumia nguvu kidogo kujitoa kwa Leythan,hapo ndipo alipopata upenyo wa kuchomoka.
“Sikubali,huyu mtoto huyu.Kama Twigaaa.Mpaka kielewe leo.Afe mtu afe Mmasai shuka libaki”
Leythan alijisemesha na kuendelea kumtizama Jemima aliyevalia kimini kifupi na kufanya mapaja yake meupe yawe nje.Akatingisha kichwa na kutoka nje.
*****
“Listen to me my fr…”(Nisikilize)
“No you listen to me Santiago,i need her now.And i don’t care how she is going to get here.I think you know what will happen to you i…”(Hapana wewe ndiyo unisikilize mimi Santiago,ninamuhitaji sasa hivi.Sijali atafikaje hapa,nadhani unajua nini kitakachokutokea....)
“But Aidan you hav…”(Lakini Aidan unatak...)
“I was brief and clear,i think this conversation is over”(Nilifupisha na kueleweka,nadhani haya maongezi yamekwisha)
Kifua cha Mzee Aidan Waytte kilikuwa kinawaka moto,alishaelewa tayari kuwa Sonia hakufa na yupo hai.Alikuwa akiongea huku akitema chembechembe za mate.Ilikuwa ni lazima amtie Sonia mikononi mwake siku hiyo na ndiyo maana alikuwa akimfokea rafiki yake Santiago kama mtoto mdogo.Haikuwa kazi rahisi kumtuliza,Mwanaye Sebastian alikuwa ana virusi vya Ukimwi vilivyosababishwa na Sonia.Aliongea maneno hayo siku hiyo asubuhi wakiwa ndani ya gari, sauti yake ilikuwa kali na aliongea huku akitetemeka,hali hiyo ilimchanganya sana Santiago.Hakuelewa ni njia gani atumie ili amvute Sonia.
“Out of my car.GET OUT!”(Toka kwenye gari langu,toka nje)
Hayo ndiyo maneno matatu aliyotamka Aidan Wayyte kwa ukali mishipa ya shingo ikiwa imemtoka.Santiago akashuka huku akiwa na hofu.Akatembea kwa mawazo mpaka ndani ya hoteli na kuingia chumbani,ambapo hata huko alikumbana na maswali kutoka kwa Mke wake, Pendo Jonas.
“Vipi,mbona upo hivyo?”
Pendo aliuliza,akamsogelea Mme wake na kukaa karibu naye kitandani.
“Hakuna kitu mke wangu”
“Kuna kitu unanificha tafadhali niambie,una nini?”
“Sonia yupo wapi?”
“Sonia?”
Sio kwamba Pendo hakusikia,alishtuka kusikia Santiago anamuulizia Sonia.
“Ndio Sonia”
“Yupo,vipi kwani?”
“Nahitaji kuonana naye,nitampata vipi?”
“Nitampigia simu,kuna nini?”
“Nikwambie kitu”
Santiago alijifanya kutabasamu ili Pendo asihisi lolote.
“Niambie mpenzi”
“Ujue Sonia sijawahi kumuona kwa macho nahitaji kumuona hana kwa hana,si uliniambia ni kama mwanao?”
“Ndio”
“Basi nahitaji kumuona”
“Kumbe hivyo,hakuna tatizo unahitaji kumuona lini?”
“Nitakwambia,lakini mwambie akae tayari tayari”
“Sawa,nitampigia simu”

***
Tangu siku hiyo maisha ya Sonia yalikuwa ya mashaka, hakuelewa ni nani anamuwinda, ili kujitoa wasiwasi akaamua kuwaajiri walinzi watano nyumbani kwake kutoka katika kampuni ya KK Security.
“Askari umenisikia,ukiona mtu humuelewi usiku piga risasi.Mimi nitatoa maelezo kwa bosi wenu”
Ilikuwa ni kauli kutoka Kwa Sonia siku hiyo alivyopewa walinzi tena wenye mitutu,hapo ndipo alipokuwa anaishi vizuri nyumbani kwake.Mbali na hapo alitafuta mlinzi wake binafsi.Akawa kila sehemu yupo naye,Sonia alizidi kutingisha jiji kila alipoingia sehemu basi nyuma yake kulikuwa na mwanaume wa miraba sita kavaa miwani nyeusi ili kulinda usalama wake yaani ‘boardguard’.Wanaume bado hawakuacha kumsumbua kila kukicha wakimpigia simu,kumtongoza.
“Sasa Salma,mbona unaitesa akili yangu lakini?”
Upande wa pili wa simu ulisikika,sauti ya mwanaume ilikuwa inamuimbisha.
“Nakutesa kivipi?jielezee mwanaume”
“Unautesa moyo wangu,nakupenda sana Salma”
“Unanichekesha ujue Fred”
“Sikuchekeshi,nakwambia ukweli.Nipo radhi kufanya chochote kwa ajili yako”
“Upo wapi sasa hivi?”
“Nipo kwangu”
“Upo na nani?”
“Mwenyewe”
“Gari yangu haina mafuta nahitaji kuja,sasa nitakujaje?”
“Nitakutumia pesa ya mafuta”
“Sina nguo za kuvaa,nguo zote chafu”
“Salma usinifanyie hivyo”
“Ndiyo nakwambia sasa”
“Nitakutumia pesa ununue”
“Sawa,tuma”
Baada ya kukata tu simu,mlio wa meseji ulisikika Sonia alikuwa amevuna shilingi laki mbili.Akatabasamu na kusonya kwa dharau.
Kabla ya kufanya lolote simu yake nyingine ikaita,alivyoangalia akagundua kuwa ni Pendo Jonas,Mama yake wa kufukia.
“Halloo Mama shikamoo”
“Marahaba,hujambo Sonia?”
“Sijambo Mama”
“Upo wapi?”
“Nipo nyumbani”
“Tunaweza kuonana leo?”
“Sasa hivi?”
“Ndiyo”
“Hakuna shaka,wapi?”
“Njoo Blue pearl hapa ubungo plaza tukutane”
“Okay Mama”
Simu ikakatwa.Hapo hapo Sonia akasimama na kuingia bafuni kujimwagia maji,akatoka na kuvaa nguo.
“Nooo Tyson.Leo ninaenda mwenyewe”
Sonia alimzuia Mlinzi wake siku hiyo wasiongozane,alikuwa ana uhakika kuwa anapoenda ni sehemu salama salmin!
***
Pendo Jonas hakuelewa kuwa anamuingiza tena Sonia kwenye matatizo,wala hakushtuka anatumiwa kama chambo amvute Sonia karibu ili atiwe mikononi na Mzee Aidan Waytte.Ilikuwa ni saa tisa alasiri Aidan Waytte alipaki gari ng’ambo ya barabara akiwa na watu wengine wa kazi aliowakodi,bado alimchukia Sonia.Alimuona Pendo Jonas na Santiago upande wa pili wakiwa kwenye mgahawa!


Njia ya kutokea Sinza kuelekea Shekilango ilikuwa na msongamano wa magari kuliko kawaida,daladala zililazimika kutanua ili kukwepa foleni na kuwawaisha abiria kwa kufanya hivyo ilikuwa ni kwenda kinyume na sheria za barabarani hiyo ikapelekea wengine kupigwa bao na matrafiki,sio njia ya kutokea mjini au kwenda katikatika zote zilifunga.Nusu saa lizima Sonia alikuwa Sinza Makaburini nyuma ya usukani gari yake unaunguruma,akitokea nyumbani kwake Mikocheni ‘B’ hakuna kitu alichochukia kama foleni.Alishapigiwa simu karibia nane kutoka kwa Pendo akimsihi afanye upesi.
“Foleni Mama,hata haitembei sijui kuna nini leo”
Hilo ndilo lilikuwa jibu la Sonia kila alipopokea simu kutoka kwa Pendo.Simu yake nyingine ikaita.
“Halloo Fredi”
“Vipi,ushatoka nyumbani?”
“Ndio,vipi kwani?”
“Ndio unakuja kwangu au?”
“Hapana kuna mahali napitia lakini nitakuja”
“Sasa Salma mbona hivyo?Nimekutumia pesa ya mafuta ili uje sasa hivi”
“Sikiliza basi,nakurudishia pesa yako maana ishakuwa kero”
“Basi yaishe unakuja saa ngapi?”
“Nitakupigia kuna sehemu napita mara moja”
“Poa”
Nusu saa lingine lilipita bado magari hayakusogea,Sonia akashindwa kuvumilia nyuma yake kulikuwa na gari ndogo aina ya Mark II,akachungulia ‘site mirror’,akaona kuna nafasi akarudi nyuma kidogo na kukunja kushoto.Alifatisha daladala iliyokuwa imempita,nayeye akaunga nyuma,hakutaka kuchelewa kiasi hicho hakufika hata mita saba akaona jopo la polisi wa usalama barabarani wamevaa nguo nyeupe.Akapigwa mkono kuwa aweke gari kando.Na ndiyo ivyo ilivyotokea kwenye costa ya mbele yake.
Askari akalifikia gari lake,akashusha kioo.
“Una haraka sana ,eti?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa askari.
“Nina haraka ndiyo afande,kuna mgonjwa namuwahi”
Akadanganya.
“Sasa hapa ndiyo umefika?”
“Hapana”
“Alafu hujafunga mkanda,nipe leseni yako”
Sonia akavuta mkoba wake kiti cha kushoto akatoa leseni yake na kumkabidhi askari.
“Sonia Nickson Shayo,mbona hauna leseni hapa,hauna leseni hapa Exipiring date inaonesha mwezi uliopita.Nipe kadi ya gari”
Askari akazidi kukagua Landcrusier Rexas ya Sonia akapita mbele ya kioo na kutizama stika,gari ilikuwa na makosa mengi kupita kiasi.
“Fire extinguisher stika yake iko wapi?Naona insurance nayo hakuna kitu, aisee wewe dada embu shuka ndani ya gari.Bima hujalipia.Shuka ndani ya gari twende pale”
Sonia alijihisi ni mdogo tangu aendeshe gari hakuwahi kuangalia vitu kama hivyo yeye ni kuwasha na kuondoka zake.Siku hiyo ndiyo ilikuwa yake.
“Wewe ni mahakamani kwa makosa yako”
“Afande njoo tumalizane”
“Hapana,huwezi kumalizana na mimi”
Sonia alivyojaribu kutoa elfu kumi ili kumuhonga ilikuwa ndiyo kwanza anajiharibia.
“Unataka kunipa rushwa?twende huku..Afande Kombe”
Afande akamuita mwenzake,Sonia alijikuta yupo kwenye makosa mengi kupita kiasi.Ilikuwa ni lazima alipe faini kubwa au akalale kituo cha polisi.
“Hawa ndiyo wakwepa kodi hawa,dada unaendeshaje gari kama unaendesha baiskaeli?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa afande mwingine,Sonia aliuchukulia huo ni kama upotevu wa muda,hakuelewa kuwa ni Mungu aliwatumia askari kama kumtoa katika hatari aliyokuwa anaifuata.
“Inabidi twende kituoni tu”
Ni kweli haraka zake zilimponza,askari wa usalama barabarani walichachamaa siku hiyo balaa.Wakaingia ndani ya gari safari ya kuelekea kituoni ikaanza.

Muda wote Sonia alikuwa akisonya kitendo hicho kilimkera kupita maelezo yaliyojitosheleza.Wakafika kituo kidogo cha polisi Sinza, wakaweka gari pembeni Sonia akaitwa ili aandike makosa yake yote.
Na ndicho alichokifanya.Hata baada ya kuandika alizidi kucheleweshwa ingawa alilipa faini tayari.
“Afande naomba funguo niende si nishamaliza kila kitu”
“Embu subiri dada,haya mambo hayaendi kienyeji enyeji”
“Bado nini?Wakati saa kumi na mbili hii.Mimi nachelewa”
“Unaelekea wapi?”
“Ubungo Plaza”
“Kumbe haukuwa na Mgonjwa, anyway utanipa lifti uniache Shekilango pale”
“Sawa,nina haraka lakini”
Nia ya askari kumchelewesha Sonia ilikuwa apate lifti ndiyo maana alijizungusha na mambo yasiyoeleweka.
Sonia akakabidhiwa funguo zake,wote wakaingia ndani ya gari.
“Sonia,mimi naitwa Afande Miraji”
“Ahsante kwa kukufahamu”
“Samahani kwa yaliyotokea pale nilikuwa kazini sikuwa na jinsi,si unajua tena mambo ya kazi”
“Usijali wala nini,naelewa”
“Samahani umeolewa?”
Lilikuwa ni swali la nje ya mada lililomfanya Sonia ashtuke na kumuangalia askari huyo mwenye kitambi kikubwa kama katuni wa kuchorwa kwenye magazeti.
“Hapana”
“Sio kweli binti”
“Sina sababu ya kukudanganya”
“Sasa unaenda kufanya nini Ubungo Plaza?”
“Kumuona Mama yangu”
Kuanzia hapo maongezi ya afande Miraji yalibadilika,tangu aanze kazi yake ya uaskari hakuwahi kukutana na mwanamke mzuri kiasi hicho wakati mwingine alidhani ni jini,uzuri wa Sonia ulizidi.
Akajaribu kumchombeza.
“Ninaweza kupata namba yako ya simu.Tukutane siku moja tupigepige stori”
“Namba yangu?”
“Ndio”
“Sawa,nitakupatia”
Sonia alimsikitikia askari huyo,alishaelewa ni kitu gani anakihitaji aliwaurumia sana wanaume.Hakuelewa ni kwanini wana tamaa kiasi hicho,kwa afande Miraji kwake ilikuwa ni kama bahati ya mtende moyo wake ulimwenda kasi hakuamini kuwa mambo yangekuwa marahisi kiasi hicho.Sonia akatoa namba za simu.
Muda ulikuwa umekwenda tayari ilikuwa imegonga saa moja ya jioni na ndiyo wakati huo walifika Shekilango,afande Miraji akashuka ndani ya gari, hakuamini kama alipatiwa namba za simu,akili yake ilimtuma kuwa alipewa namba za treni, kabla ya kuvuka barabara alitoa simu yake na kujaribu kuzipiga, simu ikaita.
“Halloo,Sonia”
“Haloo nani mwenzangu?”
Upande wa pili wa Simu ulisikika hapo ndipo afande Miraji akaamini kuwa namba zilikuwa zenyewe hazikuwa ‘fake’
“Mimi Afande Miraji,umenishusha hapa sasa hivi.Ahsante sana”
“Usijali”
Simu ikakatwa.
Alivyofika Ubungo plaza,alimtafuta Pendo Jonas hewani ili kujua ni wapi wakutane lakini cha ajabu simu haikupatikana,akajaribu tena lakini hali ilikuwa ileile.
“Sasa watakuwa wapi?”
Akajaribu kuangalia huku na kule kumtafuta lakini hakuona mtu yoyote.
“Dada naomba niletee sprite ya baridi”
Sonia akaagiza kinywaji na kukaa ndani ya mgahawa ili apunge upepo huku akimsubiri Pendo Jonas ambaye walikuwa na mihadi ya kukutana siku hiyo.
****
“Hapana Joram,sio kweli unanidanganya ili ujiteteee”
“Ukweli ndiyo huo nakwambia”
“Haiwezekani siwezi kuishi nawewe tena”
“Consolatha”
“Niachie,sikutegemea kama ungeniua”
“Nashindwa kuelewa imekuwaje”
Ulizuka ugomvi mkubwa sana ndani ya ndoa ya Bwana na Bibi Joram Wanguba,kila mtu hakuelewa ukimwi ulitokea wapi.Sababu walikuwa waaminifu kupita maelezo,japokuwa Consolatha alimuamini mume wake lakini habari alizopokea siku hiyo zilimchanganya akili yake.Hakuna ugonjwa aliouogopa katika maisha yake kama Ukimwi na leo hii anao.Alilia machozi mpaka yakamkauka akimlaumu mume wake kuwa amemuuwa.
“Consolatha”
“Si ungeniambia sasa kuliko kuniua”
Zilikuwa ni lawama alizotupiwa Joram,hata yeye alichanganyikiwa sababu hakuwahi kutoka nje ya ndoa yake hata siku moja.Na alikuwa muaminifu tangu alipompata mwanamke huyo,hakuwahi kuijua nguo ya ndani ya mwanamke mwingine isipokuwa ya Consolatha,ni bora angelaumiwa kwa kitu kilichokuwa cha ukweli.Kapu la lawana lilikuwa kwake,Consolatha aliendelea kulia akiwa chumbani.
“Conso”
Alimsogelea mke wake na kumshika lakini mkono wake ulitupwa mbali.
“Najua hutoniamini lakini naomba nikwambie kuwa sielewi,hata sijui.Labda wewe mwenzangu”
“Unasemaje Joram?”
Consolatha akageuka kwa ukali macho yake yakiwa yamemvimba kwa kulia,alielewa jinsi gani ugonjwa huo unavyouwa vibaya sana.
“Mke wangu”
“Jor..am ni..ache”
Kilio hakikukoma,Bado Joram aliendelea kuwaza na kuwazua.Alimuamini sana mke wake lakini akili nyingine ilimtuma kuwa wenda ukimwi huo uliletwa na mke wake ingawa hakutaka kuyapa mawazo yake kipaumbele. Sababu hata siku moja hakuwahi kumsikia wala kumuona mke wake ana mazoea na mwanaume yoyote yule hiyo ndiyo ilimchangaya akili zaidi,mbali na hapo hata yeye alitetemeka ndoto zake aliziona zimezimika kama mshumaa uliopulizwa na upepo.
Alikaa kitandani na kujikunyata,akajikita kwenye mawazo.
“Itakuwa saluni pale siku ya harusi,yule kinyozi alinikata.Nina uhakika huo,Eh Mungu kwanini hivi?”
Joram aliwaza akiwa mnyonge,alimuonea huruma sana mke wake aliyekuwa analia mfululizo.
“Haraka zangu ziliniponza kwanini sikuwaambia wachemshe mashine kwanza”
Majuto ni mjukuu siku zote,hivyo ndivyo ilivyokuwa.Haraka zake zilimponza.

****
Mazoea ya Sebastian na Nasra yalichepua siku hadi siku,hawakupitisha lisaa bila kuwa simuni wanazungumza na hata hawakuweza kukaa siku mbili bila kuonana,walifurahi kujuana na kila wakionana kila mtu hakukosa stori huyu aliisifia Marekani na yule aliinadi Tanzania.Kila mtu alimuhadithia mwenzake mandhari ya nchi yake.Nasra katika maisha yake hakuwahi kuvuka boda yaani kwenda nje ya Tanzania ndiyo maana alijenga urafiki na Sebastian wa karibu, aliamini siku moja ataenda Marekani na hivyo ndivyo Sebastian alivyomuhaidi.
“Nitafurahi sana nikienda Marekani,sitorudi ng’oo”
Nasra alikuwa simuni anazungumza na Sebastian Usiku.
“Hahahaa kwanini usirudi wakati unasema Tanzania ni nzuri”
“Hata kama”
“Na mchumba wako?”
“Ah bwana we, mimi natafuta maisha yakiwa bomba nitamuita”
“Unanifurahisha sana, nije kesho kukuona?”
“Sio mbaya lakini nitakuwa na Mustapha”
“Siku nzima?”
“Ndio,kuna sehemu tunataka twende”
“Sio mbaya tukaungana,nataka nije na wifi yako umuone”
“Poa tu,tena itakuwa vizuri sana”
“Poa,nikutakie usiku mwema”
“Nawewe pia rafiki yangu”
Aina ya maongezi kama hayo ndiyo walikuwa wakiongea watu hawa wawili.

***
Asubuhi kulivyokucha baada ya kupata kifungua kinywa Sebastian aligonga mlango wa Brenda,haikuchukuwa muda mrefu ukafunguliwa Brenda akatoa kichwa chake nje.
“Karibu Sebastian”
“Hapana,naomba ujiandae kuna sehemu nahitaji twende”
“Sasa hivi?”
“Ndio kama unaweza”
“Subiri basi hata kidogo ninywe chai”
“Usichelewe ukimaliza nipo chumbani”
Sebastian akaacha maagizo hayo nyuma,akarudi chumbani kwake kutafuta pamba za kulipuka siku hiyo,aliyokuwa anaenda kuonana na Nasra.
Hivyo ilimbidi atafute viwalo vyenye ‘swagga’akapekuwa pekuwa kabatini kutafuta ma ‘jeans’ akatoa moja safi na kuliweka kitandani na t shirt pia pamoja na kofia,akachukuwa ‘All star’ na kuweka kando.Mambo yakawa yamekamilika,hapohapo akamtafuta Nasra hewani ili ajuwe utaratibu unakuwaje.
“Wapi umesema?”
“Tutakutana Mwenge”
“Sasa mimi sipajui”
“Sio mbaya si uliniambia mchumba wako ni Mtanzania?”
“Ndio”
“Upo naye hapo?”
“Anaoga”
“Basi akitoka,utaniambia nimuelekeze”
“Hakuna shaka”
“Poa”
Simu ilivyokatwa kazi ya Sebastian ilikuwa ni kuweka nguo mwilini, hakuelewa ni kwanini alikuwa na furaha kiasi hicho,akavaa kila kitu mpaka viatu.Dakika tano baadaye Brenda alitoka chumbani akiwa keshajiandaa tayari.
Nasra akapigiwa simu ili atoe maelekezo.
“Ndio,napafahamu hapo kivulini?Kwahiyo wapi sasa?Mlimani city?Sawa poa poa”
Brenda na Nasra ndiyo walikuwa simuni.Ilibidi Sebastian ampatie simu ili wazungumze sababu alikuwa mgeni wa jiji la Dar es salaam.
Wakatembea wote mpaka kwenye maegesho ya magari wakaingia ndani ya Marcedez benz na safari ikaanza,Brenda ndiyo alikuwa ana kazi ya kumuelekeza Sebastian njia.
***
Hali ya Mustapha ilikuwa nzuri na mguu wake ulipona ndiyo maana siku hiyo alitaka kutembea na kuzunguka mjini na mpenzi wake Nasra,Siku hiyo waliivunja walitaka kutanua na kufanya ‘shoping’mbali mbali za nguo.
Mlimani city ndipo walipoamua waanze napo ndiyo maana walikuwa njiani maeneo ya Ubungo wakitokea Kijichi.Ni kweli Mustapha alidhamiria kumuoa Nasra kwa hali na mali.
“Huyo rafiki yako keshafika?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Mustapha baada ya taa za kijani kuruhusu na kuanza kuliondoa gari ubungo mataa.
“Mara ya mwisho wameniambia wapo My fea,Mikocheni”
“Watakuwa wamefika maana foleni hii ndiyo imetuweka”
“Hapana ninavyomjua Sebastian angenipigia simu, sid…”
Kilimchomkatisha kuongea ni baada ya simu yake kuita,alivyoangalia juu ya kioo alikua ni Sebastian.
“Ndiyo huyo anapiga,nadhani wamefika”
“Pokea mwambie tunakaribia kufika”
Ni kweli Sebastian alikuwa keshafika anawasubiri.
***
Vitu viliisha ndani ya friji lake na vilihitajika sababu alikuwa akijipikia mwenyewe,asubuhi ya siku hiyo Sonia aliamua kuwasha gari na kwenda Mlimani City ili kununua vitu vya jikoni,akiwa ndani ya gari aliendesha huku akiwa na peni pamoja na karatasi.
“Nyama,mikate,Jam,Blue band,Mayonize.Royco Mchele na unga…”
Sonia alikuwa akihakikisha vitu vyake vya jikoni na vingine aliviongezea baada ya kukumbuka,aliingia Mlimani city na kuweka gari karibu kabisa na geti akashuka na kuanza kutembea harakaharaka kuingia ndani ya jengo kubwa lililokuwa na kila kitu ndani.
Kutokana na mambo kutulia, siku hiyo hakuwa na mlinzi wake nyuma alienda mwenyewe sababu aliamini angerejea nyumbani kwake mapema.Ghafla katika kukunja kona katika duka la ‘Shoprite’ akawa amegandisha macho yake kuna mtu alimfananisha.
“Hee,Sonia”
Nasra ndiye alikuwa wa kwanza kumkumbuka.
“Nasra sio?”
“Yeah,za siku nyingi.Pole na matatizo”
Matatizo waliyopitia msituni Madale ndiyo yalifanya wajuane majina.
“Vipi unafanya nini hapa?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Nasra.
“Nimekuja kununua vitu vya jikoni”
“Mwanamke kupika,nipo na Mustapha”
“Jaaamani,alipona?”
“Ndiyo”
“Mungu mkubwa kwa kweli”
“Subiri umsalimie,nimewaacha hapo nyuma”
“Yupo na nani?”
“Rafiki yangu fulani hivi na Mchumba wake”
Hazikupita hata dakika mbili,Mustapha akatokeza akiwa na mwanaume mrefu mweusi kiasi anabonyeza simu amevaa kofia,muda wote alikuwa bize na simu yake.
“Mustapha huyu ndiye yule Sonia amba…”
“Namkumbuka Sura yake,mimi huwa sisahau sura.Pole na matatizo”
“Ahsante”
Sauti ya Sonia ilimshtua Sebastian,aliyekuwa anabonyeza simu akainua kichwa chake juu.Macho yao yakagongana,Sonia alihisi anaumwa tumbo hakuelewa la kukata au la kuharisha!

***
Alihisi mwili wake umepunguwa uzito na kuwa mdogo kama mchanga,Sonia alikuwa mpole na aliogopa kupita kiasi,Sebastian alimtisha. Alimjua sana mwanaume huyo alivyokuwa ana hasira naye na kitakachofuata dakika chache alikielewa moyoni mwake.Aliogopa kudhalilishwa mbele za watu kwa kupigwa makofi, ndiyo maana akazidi kuwa mpole ghafla.
Moyo wake ulimdunda akatamani akimbie lakini akashindwa, macho makali ya Sebastian yalizidi kumuogopesha.
“Nashukuru sana naomba niwahi kuna rafiki yangu ananisubiri”
Hivyo ndivyo alivyosema Sonia na kugeuka lakini alidakwa mkono kabla hata hajapiga hatua moja.
“Upo sawa?”
Mustapha ndiye aliyemzuia sura ya Sonia ilimfanya ahisi kuna kitu kinaendelea,kisichokuwa cha kawaida.
“Yah”
“Kweli?”
“Ndiyo!”
Bado Sebastian alikuwa na hasira na Sonia,hakuelewa amfanye nini, alizidi kumtizama kwa macho makali mno.Akamuona jinsi gani anavyohaha.Sonia hakuweza kumuangalia Sebastian usoni,aliogopa mno.Sura ya Sebastian ilijawa makunyanzi.Kilichowakatisha ni baada ya Brenda nayeye kutokeza,alishtuka kumuona Sonia,alielewa nini kitakachoendelea dakika chache zijazo, alishajua ni jinsi gani watu hao walivyokuwa maadui wakubwa hawapikiki chungu kimoja,ndiyo maana akamshika Sebastian mkono akijaribu kumzuga!
“Sebastian”
“What?”(nini)
Akaitikia lakini macho yake yote yalikuwa kwa Sonia anayeangalia chini kwa hofu.
“You shou…..”
Kabla ya Brenda kumalizia anachotaka kusema,Sebastian akachomoka kama chui na kumvaa Sonia.Akamkamata shingo na kumsukumiza,akamsogelea tena na kumtandika makofi.Kabla ya kumrushia kofi lingine Mustapha akamshika kwa nyuma.
“Stay away from this,Stay away from this i said”
Sebastian aliongea kwa ghadhabu akimwambia Mustapha kuwa ayaache mambo kama yalivyo,bado alikuwa na vita na Sonia.Alijisikia kumuuwa hapohapo,alizidi kujitoa mikononi mwa Mustapha,watu walianza kukusanyika na walinzi wa jengo wakasogea karibu.
“Kuna nini hapa?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa mlinzi baada ya kufika eneo la tukio.
Sebastian hakujibu chochote badala yake aliwapanguwa watu kwa hasira na kuanza kutembea harakaharaka akitafuta lango kubwa.
Maswali makubwa yalizuka vichwani mwa Mustapha na Nasra,hawakuwa na mtu wa kumuuliza sababu Brenda alikuwa nyuma ya Sebastian anamfuata nje.
“Sebastia…n Sebasti..n”
Sebastian hakuitikia,bado alikuwa anamtafuta Sonia hakuelewa ni wapi amekimbilia,alitupa macho yake huku na kule huku akihema kwa hasira,baadhi ya watu walimfuata nyuma kama nzi.
“Nasra,unajua chochote?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Mustapha akimuuliza mpenzi wake,Nasra.
“Embu twende,mimi nashindwa kuelewa”
Mustapha na Nasra na wao wakatoka nje,ambapo walimkuta Sebastian anaangaza huku na kule ana mtafuta Sonia.Chuki aliyojenga ndani ya moyo wake ilikuwa kubwa sana.Ungeambiwa kuwa watu hawa walipendana sana kamwe usingekubali.

****
Kitendo cha kumuona Sebastian kashikwa tu akachomoka kama sungura,aliamini huo ndiyo ulikuwa mwanya wa kuyaokoa maisha yake.Kubaki eneo hilo kulimaanisha kupigwa hata mpaka kufa.Alimjua Sebastian nje ndani.Alimuelewa kuwa ni mwanaume asiyekubali kushindwa kitu na mkorofi, mbali na hapo alijua vita yao haitoisha milele ndiyo maana alimuhofia,kitendo cha kusimama na kukaa sawa aliwapangua pangua watu na kuingia ndani ya duka la nguo akajificha.Mpaka Sebastian anapita na kutoka nje alimuona.
“Dada”
Msichana wa dukani alimuita Sonia,alimuonea huruma tukio zima lililotokea aliliona.
“Kwanini usishtaki polisi sasa,huyo bwana sio wa kuishi naye.Atakuja kukuuwa,ni mumeo?”
Msichana wa dukani alijaribu kutoa ushauri lakini hakuelewa lolote.
“Naomba nisaidie kitu kimoja”
“Kitu gani?”
“Gari yangu,nimeiacha kule nyuma nataka niondoke nisionekane”
“Pitia mlango wa kule mbele”
“Napita wapi?”
“Pita huku”
Sonia alioneshwa njia,akaanza kutembea, kuendelea kubaki Mlimani City kulimaanisha usalama wake kupotea,hakuwa na amani tena.Sebastian alimtisha.

Alitembea kwa kujihami na kujongea kwa tahadhari ambapo bado aliendelea kumuaona Sebastian anaangalia huku na kule.Alivyopita nyuma yake akaanza kukimbia.Watu wengi walimshangaa na kumnyooshea vidole lakini hakujali,alichojali ni usalama wake tu.Alitembea mpaka mlango wa pili akachungulia kabla ya kutokeza.
Alimanusura Sebastian amuone, isingekuwa mtu aliyekuwa anapita mbele kumkinga basi ingekula kwake.Moyo wake ukazidi kupiga kwa nguvu,akajishauri ni kitu gani akifanye.Akachungulia tena.

Zilikuwa ni mita kumi tu kutoka alipo mpaka kwenye gari lake na akili yake ilimtuma aingie na kutimua mbio.Siku hiyo alikuwa kama mwanajeshi anayepambana vitani,akabonyeza rimoti ya gari ili kutoa ‘lock’.Hilo ndilo likamshtua Sebastian akaliangalia gari lililopiga kelele.Kama Mkuki Sonia akachomoka,hapo ndipo Sebastian akamfuata nyuma mbiombio.Ilikuwa kama Mungu akawahi kuingia ndani ya gari kabla ya Sebastian kumfikia na kutia ‘lock’ milango.
“Open the fuc***ng door”
Sebastian alifoka akiwa nje akigonga gonga kioo cha gari baada ya kufika,akang’ang’ana na kitasa cha mlango.Sonia alizidi kutetemeka akiwa ndani ya gari.Mikono yake ililowa jasho japokuwa aliamini Sebastian hakuwa na uwezo wa kuingia ndani ya gari lakini alitetemeka ndio maana hata alipojaribu kuingiza funguo kwenye ‘switch’zikadondoka chini,Sebastian alimtisha.
Akaziokota na kuzichomeka kwenye ‘Switch’ akazungusha funguo, gari likawaka.Bila kujiuliza mara mbili akavuta gia mpaka kwenye herufi ‘R’ akarudi nyuma kwa kasi,alivyoamini gari limekaa sawa akarudisha gia herufi ‘D’ akalitoa mbio.Hiyo haikufanya Sebastian amuachie,alimuona akikimbia mpaka kwenye Marcedez Benz kibanda wazi tena bila ya kutumia mlango aliruka kwa juu na kukaa juu ya kiti nayeye akawasha gari haraka,jinsi alivyolitoa kila mtu alibaki kinywa wazi.Hiyo ndiyo ikamfanya Sonia aogope zaidi.Hakuelewa ni wapi atokee.
“Anco Dustan”
Huyo ndiye mtu pekee aliyeamini angekuwa msaada kwake,alivyotoka tu getini akachukuwa simu yake ya mkononi.Akajaribu kutafuta jina la Dustan.
“Anco Dustan,Anco Dustan,Anco Dustan”
Sonia alijisemea huku akizidi kutafuta majina, kutokana na presha aliyokuwa nayo hakuweza kulipata jina hilo kwa haraka,kilichomchanganya akili yake ni baada ya kupiga jicho kwenye ‘site mirror’ ya kulia akaliona gari la Sebastian linavyokuja kwa kasi ya risasi.Alichofanya nayeye ni kunyoosha mguu gari ikazidi kwenda mbio.Alivyopata namba ya Dustan hapohapo aliipiga.
“NAMBA YA SIMU UNAYOPIGA HAIPATIKANI KWA SASA,TAFADHALI JARIBU TENA BAADAYE”
Kauli hiyo ndiyo ilimchanganya akili yake kwa kiasi cha kutosha,Dustan hakuwa hewani.Akakosa matumaini,hakuwa na mkombozi mwingine yoyote yule.Hakuna kitu alichokifanya cha hatari kama kupanda tuta la katikati, kutokana na gari lake kuwa juu ilikuwa kazi ndogo,baada ya kunyoosha kuelekea kwake Mikocheni ‘B’ aligeuka na kurudi Ubungo.
Marcedez Benz ya Sebastian ilikuwa ni gari ya chini alivyotaka kuiga kupanda tuta,bampa liligota ikashindikana akakanyaga ‘clutch’ na kubadili gia, akarudisha gari kinyumenyume.Akalishuhudia gari la Sonia upande wa pili linazidi kumuacha.
“Son of a bitch”
Sebastian hakuwa mwanaume wa kukubali kushindwa,akaliweka gari sawa baada ya kuona ‘U turn’ mita tano mbele yake,akanyoosha mpaka alivyoifikia.Jinsi alivyolizungusha gari isingekuwa kukaza mikono gari ingemshinda na kumuhamisha barabara,alikuwa katika kasi isiyokuwa ya kawaida mpaka ikafanya gari ilalamike na kupiga kelele.

Sonia nayeye alipata akili mpya,gari alilokuwa nalo aliamini kuwa ni kubwa na lina uwezo wa kukimbia zaidi ya mara mbili ya gari alilokuwa anatumia Sebastian,akawasha ‘Turbo’ iliyokuwa na kazi ya kuipa gari nguvu hapo ndipo gari ikazidi kutembea kwa kasi,hakuwahi kukimbiza gari kama siku hiyo.
Jinsi mshale wa mwendo ulivyokuwa unaonesha hata yeye ikamuogopesha.
Kilichomchanganya akili yake hakuelewa ni sehemu gani anaenda.Alikunja kona ya kushoto alivyofika maeneo ya ‘Supastar’ akazidi kukanyaga mafuta na kuyapita magari mengine,jinsi alivyotimua vumbi nyuma iliogopesha,mawe madogomadogo ndiyo yalikuwa yanaruka.
“Mungu wangu!”
Msongamano wa magari ulimtisha,alivyoangalia kulia aliona barabara ya vumbi akalala nayo.
Bado Sebastian aliendelea na mwendo uleule wa kukimbiza gari,alibadilisha gia mpaka namba tano.Lakini aliona gari haikimbii hata kidogo,alitamani ipae amfikie Sonia.Kila Sonia alipopita nayeye alienda naye,kwa mbali alimuona anaingia barabara ya vumbi nayeye akaingia tena bila kushusha gia.
Alipunguza mwendo na kusimama baada ya kufika mbele na kuona njia mbili kulia na kushoto.Hapo ndipo alipochanganyikiwa hakuelewa Landcruiser Rexas aliyokuwa anaendesha Sonia imeelekea upande gani.
“Excuse me!”
Sebastian akamuongelesha ‘sister doo’ aliyekuwa anapita kandokando yake,akamgeukia.
“Have you seen any car passing here?Landcruiser black in colour five min…”
“Nop”
Msichana huyo alivyojibu kifupi akazidi kutembea lakini Sebastian akachomoa pochi na kutoa dolla mia mbili.
“Two hundred dollars”
‘Sister doo’ akageuka,pesa alizoziona zilimshtua moyo.
“Yeah,I have seen it”
“Where?”
“This way”
“Thank you”
Sebastian akamkabidhi pesa,akaingia ndani ya gari akakunja kushoto na kuongeza mwendo.
****
Sonia hakuelewa ni wapi anaenda,yeye aliamini kuwa atatokea njia nyingine kubwa ili azidi kusonga mbele ndiyo maana akazidi kukanyaga mafuta.Aliamini tayari amempoteza Sebastian.Hakuna kitu kilichomvuruga kama kuona ukuta mkubwa mbele yake kumaanisha kuwa hakuna njia mbele,ilikuwa ni lazima arudi alipotoka.Hapo ndipo akapata wazo la kurudi nyuma.Kabla ya kufanya hivyo nyuma aliona vumbi zito linatimka,kwa mara ya kwanza hakuelewa.Alivyoangalia vizuri aliona Marcedez benz inakimbia kwa kasi kumfuata alipo,hapo ndipo alipojua amekwisha,akageuza gari harakaharaka.
Tayari Sebastian aliona gari la Sonia na ndiyo maana alizidi kutembeza gari mbio,akapiga breki za ghafla matairi yakajishika gari lake likazunguka likapiga msele,jinsi alivyoweka gari lake ilimfanya Sonia asiweze kupita.Hapo ndipo aliposhuka mbio mbio mpaka kwenye mlango wa gari la Sonia.
“Get out,get out bitch.You think i’m joking”(Toka nje,toka nje Malaya.Unadhani natania)
Bila kujiuliza mara mbilimbili Sebastian aliokota kokoto kubwa na kuvunja kioo cha gari la Sonia.Chengachenga za vioo zikarudi na kumkata vibaya sana Sonia Usoni.Sebastian hakujali,akapitisha mkono wake ndani na kutoa lock,akamtoa nje ya gari na kumtupa nje,Sonia akateleza na kufikia mgongo,akalala chali.
****
Leythan aliamini kwamba angemkosa Jemima angepata dhambi kubwa sana,alimtamani kingono na ndiyo maana alikuwa anatumia kila njia ili amshawishi japo wapate mawasiliano ya simu,hata alivyotoka chooni alijificha nyuma ya watu ili azidi kumstadi.Akabana nywele zake vizuri kwa nyuma zilizokuwa ndefu mno,akamtizama Jemima aliyekuwa katikati anakizungusha kiuno chake mpaka chini akainuka juu na kuzidi kuchezesha nyonga zake.Kwa Leythan akawa kama fisi kaona mfupa.Akamuangalia Conie aliyekuwa kona ya mwisho hana habari anatingisha kichwa chake,hapo ndipo aliposogea karibu na Jemima mita chache tu.Alivyoona Jemima katoka nje nayeye akatoka,alivyofika kwenye kona yenye giza totoro akamshika mkono.
“Lakini shida yako nini?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Jemima baada ya kugeuka na kuiyona sura ya Leythan!
“Sikia”
“Niachie basi.Nitakui..”
“Sikiliza nikwambie Jemima,wewe ni mrembo sana.Unatakiwa kuwa na watu kama sisi.Upo na nani?”
Leythan aliongea na Jemima akiwa masikioni mwake na kila alipoongea alikuwa anafanya kama anampumulia kimahaba.
“Mimi nishakupenda,ukinikubalia.Nitahakikisha hutojuta katika maisha yako.Unajua nitakufanya nini?”
“Nini utanifanya?”
“Nitakupa mahaba yote,mimi napenda sana kulamba”
“Kulamba nini?”
“Kulamba huko chini,nitakulamba hapa mpaka ujimwagie mara mbili double”
Maneno hayo yalimchanganya Jemima,vivyweleo vyake vilimsimama.Katika maisha yake hakuwahi kufanyiwa kitu kama hicho,hakupata picha itakuwaje ndiyo maana akatulia akawa anavuta hisia.
“Nitakupaka asali,nitakuwa nilamba.Niambie sasa”
“Njoo kesho barabara ya Mtwapa,Galaxy club.Nitakuwepo kesho”
“Weka namba hapa”
Leythan akatoa simu,Jemima akaandika namba zake za simu.Kama umeme akamvuta karibu mdomoni mwake,Jemami hakuwa na uhakika kwa kitu anachotaka kukifanya ndiyo maana akasita lakini alivutwa taratibu akajikuta anafumbua mdomo wake ulimi wa Leythan ukapenya ndani wakaanza kunyonyana ndimi kwa kama sekunde kumi kisha wakaachiana.
“Tomorrow,Galaxy club”
Jemima akasema huku akimwangalia Leythan kwa macho yaliyolegea,denda alilopigwa lilimpagawisha.
Leythan alijihisi mshindi moyoni,akajiona yeye kidume cha mbegu akatabasamu na kumkonyeza Jemima, alivyogeuka akamuona Conie anatizama huku na kule.
“Ulikuwa wapi?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Conie.
“Nilikuwa chooni”
“Sasa hapa ndiyo chooni?”
“Vipi kwani?Twenzetu au?”
Leythan alibadili mada.
“Kuna Malaya wako anakuulizia”
“Malaya wangu?”
“Ndio”
“Nani?”
“Twende ukajielezee mwenyewe huku”
Mombasa alishatembea na wanawake wengi swali la Conie lilimchanganya akili yake,hakuelewa ni mwanamke gani anayetaka kuharibu starehe yake.Wakatembea mpaka meza waliyokuwa wamekaa mara ya kwanza ambapo alikuwa amekaa mwanamke mwenye rangi ya maji ya kunde.
“Oh Leythan mambo”
Hakuna hata mmoja aliyejuwa jina hilo Mombasa.Ndiyo maana akamuangalia juu mpaka chini, katika kumbukumbu zake hakuwahi kumuona mwanamke huyo.
“Poa,sijui tunafahamiana?”
Leythan aliuliza huku akimkazia macho.
“Mimi nakufahamu,naitwa Maria”
“Tulionana wapi?”
“Rafiki yake Swedi”
“Swedi gani?”
“Wa Mbagala”
‘Data’ za Leythan zote zilikuwa kichwani mwa Afande Maria na hakutaka kutumia nguvu kumkamata,ndiyo maana alijifanya kwanza anamfahamu, hakuelewa mwanaume huyo kajipanga vipi.
“Mimi siyo Leythan”
Wakati maongezi hayo yanaendelea Conie alikuwa makini kuyasikiliza,hakupepesa macho yake alikuwa makini kusikiliza kila nukta ya maongezi yao.
“Basi kuna mtu umefanana naye Tanzania anaitwa Leythan”
“Ahsante”
Hata baada ya Leythan kulikana jina lake,Afande Maria aliendelea kuzungumza nao akijaribu kuwazoea.
“Ngoja wawaongeze vinywaji kwenye bili yangu”
Ndani ya dakika kumi,walizoeana hawakuelewa kuwa wapo na mtu hatari na muda mfupi wangeingia mikononi mwa sheria!
***
Hakuna siku iliyotabirika kuwa ngumu kama mechi hiyo ya Brazil na Tanzania.Kila mtu alikuwa akiisubiri kwa hali na mali.Macho ya Watanzania yalikuwa kwa Partson Ngogo .Hata yeye mechi hiyo aliihofia kuliko kawaida sababu tu haikuwahi kushindwa katika mzunguko wa mpira,kitu kilichomchanganya akili timu hiyo ya Brazil ilivyowafunga Marekani magoli tisa kwa bila,Urusi 7-2.Urugwai 5-0.Hiyo ndiyo ikawafanya hata Watanzania waogope zaidi.
Hakuna mtu aliyetegemea ushindi.Yalikuwa yamesalia masaa arobaini na nane yaani siku mbili ili mechi hiyo iliyoitwa ya kimataifa ianze.
Na ilipangwa ichezewe Australia katikati ya jiji la Canberra.
“Baby nina imani utashinda tu”
Sauti nyororo ilipenya kwenye ngoma za masikio ya Partson Ngogo,akiwa mwenye mawazo.Alihisi kukata tamaa,swala lingine lililomuumiza kichwa ni habari za Ukimwi,bado moyo wake ulimsukuma akapime ngoma!
“Niombee Vanesa”
“Nakwambia utashinda,Tanzania inakutegemea wewe”
Maneno ya kumtia Moyo yalitoka kwa Msichana aliyeitwa Vannesa walikuwa wametoka nje ya lango la uwanja wa kimataifa, Armidale Airport,wakiwa wanaingia nchini Australia.
Partson alikuwa amevaa suti na koti kubwa jeusi,kutokana na hali ya ubaridi kuwa kali,wachezaji wote walianza kutoka mmoja baada ya mwingine mpaka walipokutana nje ambapo kulikuwa na basi kubwa lililokuwa linawasubiri.Partson hakuonesha kuwa na raha hata kidogo,alifikiria kupima afya yake japokuwa aliogopa mwenyewe.
“Nitapima hukuhuku afya yangu,nina Imani wana vipimo vya kitaalamu”
Partson aliwaza huku akiwa ndani ya basi anaangalia nje magorofa yalivyojengwa,kama ni kweli alikuwa na ukimwi kutoka kwa Samia aliamini hata Sonia pia angekuwa nao,mwanamke aliyetokea kumpenda katika maisha yake yote.Aliwasikitikia wanawake wengine tisa aliotembea nao kingono.Akamwangalia na mpenzi wake mpya Vanesa aliyekuwa pembeni yake.Basi kubwa na refu lililobeba wachezaji wa Tanzania lilizidi kusonga mbele na kupita miji mbalimbali,ilikuwa ni kama kilomita ishirini na nane zimebaki ili wafike mjini,Canberra.
***
“Ukweli ni kwamba,nishakupa ukimwi tayari.Namimi ndiyo Lissa,pole sana”
Sonia aliongea kwa hasira za waziwazi na kiburi juu,akiwa katika hali ya mateso.Sebastian kazi yake ilikuwa ni kumnasa makofi.
“Unasemaje wewe Malaya?”
“Kama ulivyonisikia Sebastian,nimechoka.Nimechoka kuishi maisha ya kuwindwa niuwe basi.Nishakupa ukimwi tayari”
Sebastian alijisikia hasira ajabu!
maneno ya Sonia yalikuwa ya kuchoma moyo.Akazidi kuvimba kwa hasira!akashindwa amfanye nini mwanamke huyu anayemwambia kuwa amemuambukiza ugonjwa hatari wa ukimwi!

***
Wanajeshi wa kikosi cha JWTZ walikuwa kituo kikubwa cha polisi staki shari,walishafanya uchunguzi wao na kugundua kuwa Mustapha alipigwa risasi na mmoja wa mapolisi aliyefanya kazi katika kituo hicho.Hawakutaka swala hilo kulifumbia macho japokuwa Mustapha hali yake iliendelea vizuri kiafya kwani kidonda chake kilichosababishwa na risasi kilikuwa kimekauka lakini hiyo haikuwafanya wanajeshi hawa walifumbie swala hilo macho ingawa lilikuwa dogo lakini wao walilikuza na likawa kubwa.
Landrover ya jeshi ilipiga breki nje ya kituo kikubwa cha polisi,jinsi walivyoshuka kwa mikwara iliwafanya mpaka polisi waliokuwa zamu siku hiyo waanze kurudi nyuma kwa uwoga.
“Mkuu wenu yuko wapi?”
Ni swali lililoulizwa na Meja Kayahira akiwa na gwanda za jeshi,sura yake haikuonesha kucheka.
Aliweka sura ya ukauzu.Alimtizama askari huyo aliyekuwa ana tetemeka kutokana na askari siku zote waliwaogopa wanajeshi.
“Yu yu yupo ndani,yupo ofisini kwake,lakini ana mtu”
Meja Kayahira na wenzake bila kujali wakaingia, wakasukuma mlango ulioandikwa RPC tena bila kufata utaratibu wa kubisha hodi.
“Ndiyo afande,mimi nilimwambia yule ni Mbuzi wangu lakini hakusikia.Hapa nilipo nimetoka mbali chanik….”
Mlalamikaji alikuwa mezani kwa RPC anatoa mashtaka yake,hakuweza kumalizia maneno yake sababu ya mlango kufunguliwa akageuka nyuma,akakumbana na lundo la wanajeshi sita.
“Naomba utupishe kidogo”
Rpc alizungumza na Mzee aliyekuwa analalamika mbele yake baada ya kuona wanajeshi ndani ya ofisi yake.Mzee akasimama na kuwaacha ofisini.
“Karibuni wakuu”
“Sisi hatuna mazungumzo mengi nadhani unamjua mtu anayeitwa Kelly Msagusa na Hassan Mbuya”
“Ndiyo ni vijana wangu hao,wanafanya kazi hapa”
“Unajua walipo?”
“Hapana lakini nilisikia tetesi kuwa walivamiwa na watu wasiojulikana wakauwawa”
“Una uhakika?”
“Sina sababu ya kuwadanganya”
“Sisi hatujaja kufuatilia kesi hiyo,kuna mwenzetu kapigwa risasi na hao polisi wako”
“Lini?”
“Unatuuliza sisi?”
“Wakuu mimi sijui chochote”
“Sasa sikiliza nikwambie kuna binti inasemekana walimteka akiwa kwake Mikocheni B wakampeleka Madale ili wamuuwe,unalifahamu hilo?”
“Hapana mkubwa”
“Wewe sindo mkuu wao?”
“Ndio”
“Basi tutaondoka wote”
“Kwenda wapi jamani?”
“Simama juu,simama juu”
Hakukuwa na lugha ya kubembeleza,kila kauli waliyokuwa wanatoa ilikuwa ni ya ukali tena yenye amri, wanajeshi hawakuwa na muda wa kupoteza.RPC Mpogole alianza kuona mambo yanabadilika ndiyo maana alihisi mkojo unataka kumtoka.Alivyotaka kusimama alihisi hana nguvu hata kidogo.
“Simama juu”
Hawakujali mavazi ya kipolisi aliyovaa mmoja wa wanajeshi akazunguka upande wa kiti chake na kumkwida shati,akamsimamisha juu na kutoka naye nje.
Walivyopita mapokezi hawakuongea chochote maaskari wote walishindwa kuelewa ni wapi mkuu wao anapelekwa na hakuna hata mmoja aliyejua kinachoendelea,akatumbukizwa nyuma ya Landrover ya jeshi akasokomezwa na buti la jeshi.
Wanajeshi wakaingia ndani ya gari na kuondoka zao.

****
Ulikuwa sio utani bali ni kweli,RPC Mpogole alifikishwa kambi ya jeshi Lugalo na kufungwa kwenye mti na kamba.
“Leo utatueleza kwanini mbuzi ana mkia mfupi”
“Tusifike huko ngoja niwaambie ukweli”
“Sema sasa hivi kabla hatujakukamua mavi hayo!”
“Kuna mzee wa kizungu anaitwa Waytte,ndiyo huyo aliwatuma”
“Ulijuaje?”
“Mimi ndiyo alinifuata kituoni ili nimtafutie vijana wa kazi”
“Kwanini alifanya hivyo?”
“Kwa kweli sijui”
“Mbona hukutuambia tangu kule, tumechoma mafuta yetu kukufuata?”
“Mnisamehe tu”
“Huyo mzee anapatikana wapi?”
“Sijui kwa kweli”
“Huna namba yake?”
“Aliniachia lakini sasa hivi haipatikani”
“Ni raia wa wapi?”
“Marekani”
Rpc Mpogole alikuwa akijibu maswali kama yupo kituo cha polisi,pesa alizohaidiwa kupewa zilimtokea puani hakuwahi kuwaza kuwa mambo yangemuendea kombo kiasi hicho ndiyo maana hakua na sababu ya kuweka siri yoyote kifuani sababu hakumaliziwa malipo ya pesa zake.
“M.P Dondo.Tumuachie huyu?”
Baada ya kuhoji maswali Meja Juma Araphat alimgeukia mwenzake na kumuuliza.
“Yaani aende hivihivi?haiwezekana kuna nyasi za kukata kule, kuna vyoo vichafu akadeki”
RPC Mpogole alitolewa kwenye mti na kupewa adhabu hizo.Hawakushughulika naye tena kuanzia siku hiyo, kazi yao ilikuwa ni kumsaka Aidan Waytte,waliapia kuwa ni lazima wangemfanya kitu kibaya mzungu huyo ili akawaadithie wenzake Marekani.
***
“Hapana Mr.Waytte umekaa nchini kimagendo kwa wiki tatu sasa.Viza yako imeisha wakati wake”
“Ndiyo naelewa lakini ninahitaji kuongeza siku”
“Haitowezekana,ushafanya kosa tayari hilo swala litakuwa gumu sana inabidi ulipe faini ya dolla mia tano kisha nitakupa siku mbili tu ya kukaa nchini Tanzania”
“Nisaidie bado nina kazi za kufanya hapa Tanzania”
“Haitowezakana,tafadhali jaza hii fomu kisha ukalipie benki ya ACCESS hapo nyuma,uje na risiti kesho asubuhi saa nne”
Rehema Mwaipungu aliyekuwa katika idara ya uhamiaji ndani ya ubalozi wa Tanzania hakuonesha hali ya utani,kibali cha kukaa nchini Tanzania cha Mr.Waytte na wote aliokuja nao vilikuwa vimekwisha wakati wake, hivyo alitakiwa aondoke nchini mara moja.Mama huyo mtu mzima alichachamaa tena hakumuangalia Waytte usoni,akachana karatasi za risiti na kumpatia ajaze kisha aweke sahihi yake kwa chini.
“Chukuwa hii,ili tuongee vizuri”
Mzee waytte alijaribu kupenyeza dolla elfu moja za kimarekani dirishani kisirisiri kama kubadilisha mawazo yake lakini Rehema Mwaipungu alikataa,aliogopa sana rushwa hususani kipindi hicho cha mwezi wa mfungo wa Ramadhan alichokuwa amefunga.
“Ahsante, nenda tu kalipie hizo dolla mia tano.Siku njema”
Walikuwa wametenganishwa na kioo kikubwa hivyo walitumia mikonga ya siku kufanya mawasiliano.

Mzee Waytte aliondoka ubalozi wa Tanzania akiwa mdogo kama kidonge cha ‘pilton’sababu bado alikuwa na kazi ya kufanya,Sonia ndiye alimfanya atake kubaki nchini Tanzania ili ammalize.Kitendo cha kuwa hai kiliufanya moyo wake ujawe na uchungu ajabu,aliamini kuwa hakustaili kuishi duniani hata chini ya maji pia.
“Sio mbaya,hii dunia ipo mikononi mwangu.Nitamuuwa tu kwa njia moja au nyingine”
Waytte aliapa moyoni huku akitoka nje ya geti kubwa hapo akaingia ndani ya taxi iliyokuwa inamsubiri.Alichofanya ni kumpigia Simu Santiago na kumueleza kila kitu alichoambiwa.
Hata wao vibali vyao viliisha na walitakiwa kulipa faini ya dola mia tano kila mmoja kabla ya kurejea nchini Marekani.
“Mpigie Sebastian pia,mwambie ajiandae na safari, kesho kutwa tunaondoka”Alimwambia pia mkewe simuni.
“Sawa,nitafanya hivyo akirudi nitamwambia”
“Mpigie simu sasa hivi,Olivia”
“Nitampigia”
Mzee Waytte alikuwa amevurugwa kwa kiasi cha kutosha,kutoka nchini humo bila kum-maliza Sonia aliamini kuwa ni kosa la jinai!
***
Damu ziliendelea kumtoka puani na mdomoni.Mashavu yake yalibadilika rangi na kuwa mekundu, alivimba sura nzima.Licha ya kuumuka kama hamira lakini Sebastian aliendelea kumtandika makofi yasiyokuwa na idadi kamili.
“Leo ndiyo Leo”
Sebastian alimvuta Sonia na kukipigiza kichwa chake juu ya boneti la gari,alivyomgeuza tayari alikuwa amempasua kichwa juu ya paji la uso.Sonia alihisi maumivu ya kufa na alielewa kuwa huo ndiyo mwisho wake siku hiyo.
Hakuwa na nguvu za kujitetea tena,alivyojitahidi kufumbua macho yake alikuwa anahisi kizunguzungu.
“Niu..e tu.Niu..e tu”
Hayo ndiyo maneno aliyotamka msichana huyo mrembo akiwa katika hali ya mateso ya kupigwa.Hata hivyo aliamini kama angekufa siku hiyo angemshukuru Sebastian sababu kifo kilichokuwa kinamngojea mbele yake alikiogopa,kilikuwa ni kifo cha kutisha na cha aibu kama kilivyochukuliwa na jamii.Wengi wangemuita Malaya,hakuna hata mtu mmoja ambaye angempa heshima baada ya kifo chake.

Gari la Sonia lilikuwa pembeni limevunjwa kioo,mbele ilipaki Marcedez benz nyeusi.Picha hiyo ilimuogopesha Mzee aliyefahamika kwa jina la Urrasa,aliyetoka nje baada ya kusikia vishindo vya watu.Ulikuwa ni mchana kweupe lakini ilimlazimu atoke na bastola yake ili kujihami,akazidi kusogea karibu.
Akatizama kwa karibu na kuona Mwanamke ameshikwa anapigwa vibaya sana damu zinamvuja,kwa picha iliyomjia kichwani na jinsi Landcruiser Rexas ilivyopasuliwa kioo alijua mtu anayempiga ni jambazi.Ndiyo maana akakoki bastola yake ili kutoa msaada.
“Paaaa! Paaaaaa!”
Mzee Urasa,aliachia risasi mbili mfululizo bastola yake akiwa ameielekezea angani,risasi zilienda juu.
Sebastian akashtuka kwa hofu na kuweka mikono yake hewani.
“Tulia hivyo hivyo”
“I’m not a bad guy here, do not shoot”(Mimi sio mtu mbaya,usifyatue risasi)
Sebastian aliongea akijitetea aliogopa kufa,ndiyo maana akaweka mikono juu.Sonia alikuwa chali amelala anapumua kwa mbali,kila kitu alikiona na kusikia kwa masikio yake.Mzee aliyekuja ndiye aliokoa maisha yake.
“I’m Sorry I was, i was it’s jus…”
Sebastian aliongea kitu kisichoeleweka hiyo yote ilikuwa ni hofu ya kifo cha kupigwa na risasi,alitia huruma ujanja wake ukawa mfukoni aliogopa macho makali ya mzee huyo aliyetoka na vest mwenye kitambi.Japokuwa alikuwa na kiburi lakini siku hiyo alifyanta.
“Get lost,get lost young man”
Kauli hiyo iliyotoka kwa mzee aliyesimama mbele yake ikimwambia apotee hakuiamini,akatembea taratibu mpaka ndani ya gari lake na kuingia huku akimuangalia Mzee Urasa kwa wasiwasi, akili yake ilimwambia kuwa angepigwa risasi ya kisogo.Mpaka anawasha gari bado alikuwa mwenye mashaka.Akaweka gia na kulitoa gari mkuku!
***
Kwa mara nyingine tena Sonia alikuwa amepona,aliamini bado maisha yake yalikuwa marefu kuishi duniani.Alizinduka akiwa hospitalini saa tano ya usiku na alihisi maumivu makali mno usoni mwake na shingo nzima,pembeni yake alisimama mzee mnene kiasi mwenye kitambi na mvi chache kichwani.
“Unajisikiaje binti?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Mzee Urassa,na huyu ndiye aliyemleta hospitalini vilevile.
“Nin..aendelea vizuri tu”
“Pole na kila kitu”
“Ahsante”
“Gari yako,ipo nyumbani kwangu usijali kuhusu hilo”
“Ahsante pia”
“Simu yako hii hapa,nimpigie nani sasa hivi?”
“Ha..pana usimpigie mtu yoyote kwa sasa”
“Aya ugua pole”
Sonia alizungumza kwa taabu na mateso mno,bado alihisi maumivu na alikumbuka kipigo alichopigwa masaa machache yaliyopita,mkong’oto aliopewa haukuweza kuelezeka kwa maandishi.
Bado hakutaka kuamini kwamba Sebastian ndiye kampiga kiasi hicho,kumbukumbu zake zilisafiri na kurudi nyuma,mambo mengi yakamiminika kama maji kichwani akayakumbuka mapenzi aliyopewa na mwanaume huyo akajiona yupo kitandani anatolewa bikra yake,akiamini kuwa ndiye angekuwa mume wake wa maisha,aliwaza vitu vingi sana akawa kama anaangalia filamu ya kusisimua.
Akahisi macho yake yanajaa maji yakatokeza nje ya macho na kuchuluzika mashavuni, yalikuwa ni machozi.Sonia alilia kwa uchungu bado aliamini yupo ndotoni.
Ghafla mawazo yake yakabadilika na kurudi katika ugonjwa hatari wa Ukimwi aliokuwa nao,hiyo ndiyo ilimchanganya zaidi akaanza kulia kwa sauti.
“Dada usilie”
Nesi aliyekuwa pembeni alimsogelea,Mzee Urasa alilishuhudia tukio hilo.
“Huwezi kumchoma sindano ya usingizi alale?”
Mzee Urasa alijaribu kumshauri Nesi.
“Tunaweza”
“Kwanini msifanye hivyo sababu nahisi ni maumivu yanamsumbua”
Dakika moja baadaye nesi alirudi na chupa ya dawa akachomeka bomba la sindano na kuvuta dawa,akaichoma dripu ya maji iliyokuwa kitandani mwa Sonia,hakuzikupita hata dakika tano Sonia akasombwa na usingizi mkali.
***
Sonia alificha ukweli wa maisha yake ndiyo maana akadanganya mpaka jina,hakutaka historia yake iwe wazi.Nia yake ilikuwa kujificha popote pale,akanunua busara za Mzee Urasa akajifanya ni mpole aliyeonewa.
“Ninahisi hawa ndugu zangu wanajaribu pia kuniua,baba yangu aliniachia mali nyingi baada ya kufariki kama nilivyokwambia na alizaa watoto wengi.Nyumbani ninaogopa kurudi”
“Sasa Agnes inabidi ukaishi kwangu,mpaka pale mambo yatakapotulia.Nishaongea na mke wangu.Tutakusaidia”
“Nitashukuru sana”
“Usijali”
Mzee Urasa kwake akawa kama mwavuli wake wa kujificha.Hali yake ilikuwa ya kuridhisha ingawa alipewa dawa za kumeza alivyooruhusiwa kutoka hospitali siku hiyo.
“Gari nimepaki huku,jitahidi kutembea pole sana”
Sonia hakuweza kutembea vizuri,alipiga hatua chache mno huku akichechemea kutokana na maumivu yaliyokuwa kwenye mguu wake wa kulia.Wakatoka mpaka nje na kuingia ndani ya gari la Mzee Urasa.
Dunia kwa Sonia iligeuka na kuwa sehemu ya kuwindwa,alijifananisha na kifaranga cha kuku,hata siku moja hakuwahi kuelewa ni watu gani wanataka kumuuwa na picha iliyotokea siku chache nyuma zilizopita ndiyo ikamfanya aogope zaidi.Wakati anawaza hayo Mzee Urasa alikuwa kimnya anaendesha gari.
“Ahsante sana,ahsante kwa msaada wako ni binadamu wachache sana wenye roho kama yako”
Sonia alivunja ukimya,akam-butua Mzee Urasa aliyekuwa makini nyuma ya usukani.
“Usijali mwanangu”
Mzee Urasa alikuwa mzee wa Kichaga aliyekuwa mfugaji mkubwa wa Ng’ombe na mbuzi alikuwa na nyumba kubwa iliyozungushiwa ukuta mrefu kwenda juu sana!Pia alimiliki maduka mengi ya vifaa vya ujenzi Mjini Kariakoo,alikuwa ni Mzee mwenye mke na watoto wanne tu.
Mzee Urasa alikuwa mkarimu,ndiyo maana alimsaidia Sonia akimchukulia kama mwanaye wa kumzaa.
“Piii piiiiiiiii”
Honi ilisikika nje ya geti kubwa la rangi ya kijani.
Mlinzi akatoka harakaharaka na kulisukumiza upande wa kushoto geti hilo la kisasa lililokuwa na matairi madogo kwa chini.
Gari likaingia ndani,likapaki eneo maalum,ambapo pembeni pia kulikuwa na magari mengine mawili.
“Karibu Agness,hapa ndiyo nyumbani kwangu”
“Ahsante”
Wote wakashuka ndani ya gari na mlango ukafunguliwa na Mwanamke mnene mnene aliyevalia nguo ya kitenge.
“Karibuni,karibu mgeni”
“Ahsante.Agness huyu ndiyo Mke wangu anaitwa Mama Happy”
“Shikamoo Mama”
“Marahaba Mwanangu na karibu sana jisikie upo nyumbani”
Sonia alikaribishwa pia vizuri na mke wa Mzee Urasa,akaoneshwa chumba cha kulala kilichokuwa na kila kitu ndani.

Tangu siku hiyo Sonia aliishi kama mwanafamilia,akapendwa na kupewa kila kitu.Hakuna hata mtu mmoja aliyejuwa kuwa jina lake ni Sonia,aliishi kwa Mzee Urasa kwa muda wa siku tano na kuzoeleka kabisa lakini kamwe hakuthubutu kutoka nje,mbali na hapo alibadili namba za simu pia.Hakutaka mawasiliano na mtu yoyote yule.
****
Kitu kilichomchanganya Sonia baada ya wiki moja kupita ni kimoja tu,asubuhi alikuwa akiamka anapoteza kumbukumbu zake kabisa.Alielewa hakuwa katika hali ya kawaida,alihisi kuchoka mwili mzima,mwili wake ulikuwa mzito kupita kiasi na hata kichwa huwa kinamsumbua.
“Mh!”
Siku hiyo aliamka asubuhi na kuguna,hakuwa ana kumbuka lolote lililotokea jana yake.Kila alipojaribu kukumbuka alishindwa,alihisi kuna kitu kinaendelea kichwani mwake.Alivyotupa macho yake ukutani ilikuwa imetimu saa saba za mchana na ndiyo muda huo kila siku alikuwa akiamka siku mbili mfululizo,alihisi ni lazima kutakuwa na tatizo lakini alipuuzia.
Kesho yake pia hali ilikuwa hivyo hivyo aliamka mchana wa saa saba kichwa chake kikiwa kizito mno.
“Itakuwa naumwa, lazima niseme”
Siku hiyo alimsubiri Mzee Urasa usiku arudi kazini kwa hamu ili amweleze kila kitu.Alivyosikia honi ya gari usiku wa saa mbili alijitayarisha vizuri ili amuambie tatizo lake.
Na ndiyo ilivyokuwa baada ya salamu kila kitu alikiweka wazi.
“Kwamba una poteza kumbukumbu?”
“Ndiyo!”
“Mbona unanitisha mwanangu?”
“Alafu tatizo lingine huwa nachelewa kuamka sana siku hizi”
“Itabidi nikutafutie daktari,ngoja nimpigie dokta sasa hivi aje”
Mzee Urasa hapohapo alitoa simu yake ya mkononi na kumtafuta daktari wake.
“Ndiyo njoo hapa kwangu,sasa hivi…yes ndio ndio”
Sonia alitolewa wasiwasi kuambiwa kuwa aendelee na mambo mengine kwani daktari angefika muda mfupi ili kujua afya yake kwa ujumla.
Kusikia hivyo hakuwa na wasiwasi tena,akatabasamu na kuingia chumbani ambapo alikaa macho ili kumsubiri daktari.
Saa tatu ya usiku baada ya lisaa limoja kupita akiwa chumbani alisikia kengele inalia,akatega sikio lake kwa makini.
“Karibu dokta,pita ndani”
Sauti ya Mama Happy ilipenya masikioni mwake,daktari alikuwa keshafika.Akazidi kuyasikiliza maongezi hayo kwa umakini,akisubiri aitwe.
“Ngoja nimuite Mzee muongee,karibu uketi”
“Nashukuru”
Maongezi yakazidi kuendelea,dakika mbili baadaye akasikia anaitwa.Akasimama na kufika seblen.
Baada ya kusalimiana na daktari alianza kujieleza jinsi alivyouhisi mwili wake.
“Mgongo huwa haukuumi?”
Dokta aliuliza huku akimtizama Sonia.
“Hapana kichwa ndiyo huwa kinauma kwa sana”
“Na mwili je?”
“Mwili pia unakuwa umechoka pia”
“Unasema kuwa unapoteza kumbukumbu vilevile?”
“Ndiyo”
“Hujawahi kujigonga sehemu yoyote kichwani,au kupata ajali siku hizi za karibuni?”
Lilikuwa ni swali lingine kutoka kwa Dokta,Sonia akamtizama Mzee Urasa aliyekuwa pembeni yake.
“Ndiyo aliwahi kupata ajali”
Mzee Urasa akadakia.
“Okay”
Dokta aliendelea na maswali kwa mgonjwa wake,akamchukuwa vipimo kama damu kubwa ili azidi kufanya utafiti zaidi.
“Kesho nitakuja na majibu,inabidi pia apimwe CT scan ya ubongo”
“Sawa hakuna shida daktari,wacha tusubiri majibu”
“Ahsante kuweni na usiku mwema”
***
Dokta Junior Machage,alishtuka mno vipimo vyake vilimshtua sana akashindwa kupata jibu la harakaharaka,kabla ya kutatua jambo hilo kichwani kwake.Hapohapo simu yake ikaita,alivyoitizama aligundua kuwa ilitoka kwa Mzee Urasa.
“Halloo Shikamoo Mzee”
“Najua unajua nini kinaendelea,nachokuomba ufunge mdomo wako.Yaache haya mambo kama yalivyo!”


****
Katika wanajeshi waliokuwa na Usongo wa kumtia mkononi Mzee Aidan Waytte ni mwanamke huyu M.p Magdalena John, ndiyo maana alikuwa anaendesha gari ya jeshi kama mtu aliyechanganyikiwa akili.Pembeni kulikuwa na mwanajeshi mwenzake Sirgent Peter Machabe na nyuma ya gari hilo walisimama wengine watatu,jumla walikuwa watano kujumlisha na Magdalena,muda wote alikuwa anayabana meno yake kwa hasira.Walishapata tetesi kuwa Aidan Waytte yupo njiani anaelekea uwanja wa ndege ili aondoke, niya yao ilikuwa ni kuzuia safari yake, hawakujali kuwa wangesababisha ugomvi mkubwa sana,sio kwamba hawakuelewa wanaenda kinyume na sheria bali walitumia mabavu.
“Ndege inaondoka saa ngapi?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa M.P Magdalena akimuuliza mwenzake kushoto.
“Saa sita”
“Sasa hivi saa ngapi?”
“Saa tano na dakika mbili”
Bado walikuwa wana lisaa limoja kasoro mbele ili shirika la ndege ya KLM iachie ardhi ya Tanzania Uwanja wa kimataifa Mwalimu Nyerere,hiyo ikamfanya M.P Magdalena aone kuwa wana muda finyu kwa hasira akazungusha usukani na kupanda tuta la katikati,hakujali kuwa hayupo katika njia yake.
Badala ya kupita kushoto aliingia kulia kwenye barabara ya magari yaendayo Mjini,kutokana na gari hiyo kuwa na mabaka ya Jeshi madereva wengi walilipisha wakijua kuna tatizo kubwa.
“Pipipi piiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii”
Magdalena alipiga honi za gari mfululizo,akawa anasambaratisha magari mengine.Mwanajeshi aliyekuwa pembeni yake alijishika vizuri,mwendo wa gari hilo ulimtisha.Akaingiza gari barabara ya vumbi ili kufupisha njia na kuwahi,vumbi lililotimka halikuwa la kawaida liliwafanya mpaka wakazi wa Maeneo ya Magomeni Mapipa wapaliwe na vumbi na kukohoa.
“Kuna nini jamani?Hawa wanajeshi mbona wanakimbia hivyo”
Watu waliulizana kila gari hilo lilipopita.Ndani ya dakika kumi na tisa wakatokea barabara kubwa ya Tazara,mwendo ulikuwa ni uleule na zilikuwa zimebaki dakika thelathini tu.Hiyo ndiyo ilimchanganya M.P Magdalena kupita kiasi,hakuwa na jinsi sababu mshale wa spidi uligota mwisho gari ilikuwa inakimbia mithiri ya risasi.Walivyoliona bango la Uwanja wa Ndege hakupunguza mwendo pia,mpaka alipolifikia geti.
“Ebwana tuna haraka,tukimkosa mtu wetu.Wewe ndiyo utawajibika”
Ulikuwa ni mkwara kutoka kwa M.P Magdalena baada ya kuona mlinzi anataka kufanya kazi yake ya ukaguzi.
“Sawa piteni waheshimiwa”
M.P Magdalena baada ya uzio kutolewa aliweka gia namba mbili hapohapo,na kulichomoa gari kwa kasi,alimanusura wanajeshi waliokuwa nyuma wajigonge kwenye machuma.Jinsi gari hiyo ilivyokuwa inakimbia ikawafanya macho yao yawe mekundu.
***
Mr.Aidan Waytte alichelewa kufika uwanja wa Ndege sababu ya Sebastian,alimtafuta Mwanaye kila kona na huyu ndiye aliyewafanya wachelewe.Na kama wangeachwa na ndege basi kapu la lawana angetupiwa yeye,kwa maana hiyo alianza kumlaumu kabla hata hawajafika uwanja wa ndege.
“Ninakwambia hivi,ndege ikituacha Sebastian.Utanitambua”
“Lakini Baba si yameisha,nishakuelewa”
“Kelele mpumbavu wewe”
Ndani ya taxi ya familia ya Mzee Waytte tangu wanatoka Hotelini ilikuwa vurugu mtindo mmoja,Mzee Waytte alikuwa anafoka tu.
“Lakini Baba Sebastian sio kitu kizuri kumfokea mtoto”
Mama akaingilia kati.
“Nawewe unamtetea?huyu ni mtu mzima kila kitu apigiwe kelele.Zimebaki dakika arobaini tu.Boarding pass bado hapo.Ananikera wakati mwingine”
“Baba lak..”
“Ninapoongea nawewe inakubidi ufunge hilo bakuli lako,mjinga wewe”
Taxi mbili zilikuwa zinaongozana ya nyuma iliwabeba Pendo Jonas pamoja na Mwanaye Brenda na mume wake Santiago.
Mpaka wanafika uwanja wa ndege zilikuwa zimebaki dakika chache tu.Hawakuwa na muda wa kupoteza wakatoa mizigo yao harakaharaka kwenye gari na kuanza kuburuza mabegi mpaka kwenye lango la kuingilia abiria.
“Your passport sir!”
Mkaguzi alianza kuangalia hati zao za kusafiria mmoja baada ya mmoja wakiwa wamepanga mstari Mr.Waytte akiwa wa mwisho na aliyetangulia alikuwa ni Mr.Santiago.Wakaonyesha Passport zao.Ilivyofika zamu ya Mr.Waytte kukaguliwa alihisi muungurumo wa gari usio wa kawaida,ilibidi ageuke akaona kundi la wanajeshi wanashuka ndani ya gari wakiwa na mitutu yao,hakuelewa lolote baada ya ukaguzi huo akaingia ndani.
“Tunaomba kupita”
Lilikuwa ni ombi kutoka kwa mmoja wa wanajeshi akitaka kuingia ndani.
“Passport”
“Unatupotezea muda”
Ikawa vuta nikivute isingewezekana hata kidogo kwa mtu yoyote kuingia ndani ya mlango huo kama sio msafiri.
“Hapana siwapotezei muda,hapa kuna utaratibu wa kuingia ndani tunafuata protocol.Acheni mambo ya ubabe”
“Kwahiyo,unapisha haupishi?”
“Siwezi kuruhusu hilo, nikifanya hivyo nitapoteza kazi yangu.Labda muwe na kibali maalum”
Mlinzi akaweka ngumu, hakuelewa maneno yake yalikuwa ni sawa na upotevu wa muda.
Kila abiria aliyekuwa anaondoka siku hiyo jina lake lilikuwa kwenye ‘System’Shirika la ndege ya KLM lilitoa tangazo kwenye kipaza sauti wakitaja majina ya abiria ambao hawakuwepo ndani ya ndege.Hapo ndipo Waytte,Santiago,Olivia,Brenda na Pendo walipoharakisha wakaanza kukimbia.
Ilikuwa punje kidogo geti namba kumi na mbili lifungwe ambapo wasingeruhusiwa kusafiri siku hiyo.
“Where have you been sir?”(Ulikuwa wapi mzee)
Swali hilo lilitoka kwa Muhudumu wa ndege aliyekuwa amepewa dakika mbili za kuwasubiri wateja hao ambao ni abiria,hapo ndipo lango likafungwa walitembea huku wakimshukuru Mungu.Licha ya kupata ndege Mr.Waytte alionekana akiwa na hasira mno.Kichwani mwake alimuwaza Sonia,moyoni aliapia ipo siku angerudi tena Afrika kumtafuta,hata kwa Sebastian pia, ilikuwa ni kama wanawaza kitu kimoja.
***
Madawa makali yaliyoitwa caliform clonem clotrimazone ndiyo alikuwa anatumia mzee Urasa,hakuelewa ni shetani gani alimvaa.Uzuri wa Sonia ulimtoa mate siku hiyo alivyomkuta usiku peke yake seblen anaangalia televisheni amaejiachia,sketi yake imepanda juu kidogo mapaja yake manene yapo wazi.Na ndiyo akawa anatumia madawa hayo makali yaliyokuwa anayatumia kuipa mifugo yake.
Alielewa sana kuwa dawa hizo ni hatari na kali mno,endapo zingezidishwa kipimo basi mtumiaji angepoteza maisha.
Mzee Urasa hata siku moja hakuwahi kufikiria kama atakuja kufanya kitu kama hicho tena kwa binti mdogo ambaye alimfananisha na mwanaye,kila siku alikuwa akimuwekea Sonia tone moja la dawa hiyo kwenye glasi ya maji ya kunywa ifikapo usiku muda wa kula chakula mezani.
“Mama Happy ngoja niende zizini mara moja,nikamuangalie yule ndama”
Hivyo ndivyo alivyokuwa akimuaga mke wake kila ifikapo usiku wa saa tano,Mzee Urasa aliamka na funguo nyingine za Spea na badala ya kutoka nje alitembea mpaka Mlangoni mwa Sonia kwa kunyata na kuingiza funguo kwenye kitasa.Alikuwa akaziamini sana dawa hizo kali,alipofika tu alishusha suruali na kutoa boxa yake.
Kazi yake ilikuwa ni kumuingilia Sonia kimwili kila usiku,hakuelewa kuwa yupo katika hatari kubwa ya kupata ugonjwa wa Ukimwi na alihakikisha kila alipomuingilia anampangusa na kumuacha katika hali ya usafi.
Hali hiyo ilimchanganya sana Sonia,ugonjwa alioambiwa anao ulimvuruga akili sababu hakuwahi kuwa nao kabla.
“Sidhani!”
Sonia kila siku alijiuliza maswali,kama kawaida siku hiyo alizinduka saa saba za mchana bila kuelewa lolote lililotokea,wakati mwingine alidhani wenda ni kweli.Sababu daktari alimwambia huo ugonjwa unawezekana na ni wenda alirithi kutoka kwa baba yake au Mama yake,hakuelewa kuwa alifanywa MTUMWA WA NGONO ndani ya himaya ya Mzee Urasa.
Maisha ndani ya nyumba hiyo aliyafurahiya sababu alipendwa sana akachukuliwa ni kama mmoja wa wanafamilia.
Siku hiyo usiku kama kawaida walikusanyika mezani kasoro mzee Urasa aliyekuwa jikoni,anatoa maji kwenye friji.Ndani ya dakika moja akarudi na glasi za maji juu ya Sinia.
“Mume wangu siku hizi mh,hiyo tabia yako ukiendelea nayo nitanenepa”
Mama Happy alitoa sifa.
“Ipi hiyo?”
“Hiyo ya kuandaa maji na vyakula mezani”
“Ukiona hivyo ujue nazeeka vizuri”
Hakuna hata mtu mmoja kati yao aliyejua siri ya Mzee Urasa kufanya hivyo,wao walimfurahia sana.Hata Sonia alionesha tabasamu,glasi yake ilikuwa pembeni ina maji ya kunywa,ambayo yamewekwa dawa kali za ‘Calform clenom clotrimazole’.
“Griii griiiii”
Simu ya Urasa iliita na ndiyo ikamfanya asimame kutoka mezani.
“Mwanangu naomba unisaidie na maji yako,kachukuwe mengine jikoni”
Mama Happy ndiye aliomba, akachukuwa glass ya Sonia na kunywa maji yote.Sonia hakuwa na tatizo akasimama na kwenda kuchukuwa maji mengine.
Mzee Urasa alivyofika mezani wakaendelea na mazungumzo,hakuelewa chochote.Hakuelewa kuwa maji aliyotakiwa anywe Sonia siku hiyo amekunywa mke wake!Kilichosikika hapo ni milio ya sahani ya vijiko.
“Usiku Mwema,wacha mimi nikajinyooshe”
Mzee Urasa alikuwa wa kwanza kusimama,Sonia akatoa vyombo nayeye akaingia chumbani kwake.Ambapo alijimwagia maji na kuvaa ‘night dress’.Akatembea mpaka kitandani kwake na kujitupa.

Mawazo ya hali aliyokuwa nayo yakamjia kichwani,akaanza kukosa raha.Ugonjwa aliokuwa nao aliuogopa sana na kifo kilichokuwa kinamngojea kilimtisha kupita kiasi,aliwaza vitu vingi kichwani akawaza wanaume aliowaambukiza ugonjwa huo hatari.Akapapasa mkono wake na kuvuta simu yake iliyokuwa juu ya meza,akatoa laini mpya na kuweka yake ya zamani.Jinsi meseji zilivyokuwa zinamiminika kama maji bombani ilimtisha.Kazi yake ilikuwa ni kusoma meseji moja baada ya nyingine.
“HUJAMBO?BABU YAKO ANAUMWA,TUPO MOSHI UKIPATA UJUMBE HUU NIPIGIE SIMU”
Ulikuwa ni ujumbe aliousoma kwa makini uliotoka kwa Dustan,akatafakari kidogo na kuendelea kuperuzi.Meseji nyingine zilitoka kwa wanaume wakimtongoza!
Bila kuchelewa hapohapo akaiweka namba ya Dustan vizuri na kuipa simu okay.
“Hallo Anco Dustan,shikamoo”
“Marahaba,mbona hupatikani kwenye simu nimekuja kwako nikaambiwa uliuza nyumba.Uko wapi sasa hivi?”
“Anco Dustan nitakuhadithia kila kitu”
“Tuko Moshi,Babu yako anaumwa yupo K.C.M.C anahitaji kukuona”
“Sawa nitakuja”
“Lini?”
“Hata hata hata kesho”
“Sawa,jitahidi uje”
“Ahsante Anco”
Taarifa hizo zilikuwa za kuogopesha kwake,Sonia alimpenda sana Babu yake Mzee Shayo.Kabla ya kuwaza kitu kingine chochote alihisi mlango wake unatekenywa na funguo.Kwa mara ya kwanza alidhani alisikia vibaya lakini uliendelea kuchokonolewa, ilikuwa ni kama mtu yupo nje anatumia funguo.Wasiwasi ukamuingia,akaweka simu kando haraka na kujifunika na shuka.Masikio yake aliyategesha vizuri akahisi mlango umefunguliwa ukafungwa,akamsikia mtu anatembea kumfuata alipo,marashi ya Mzee Urasa aliyatambua japokuwa hakutaka kulipa jibu la swali lake kipaumbele,alitamani kufumbua jicho moja lakini aliogopa mno.Mapigo yake ya moyo yakazidi kupiga kwa nguvu.Mzee Urasa kama siku zote anavyofanya hakuelewa kuwa Sonia yupo macho na anamsikia kila kitu kuanzia alipoingia na dawa alizompa kwa kumuwekea ndani maji alikuwa amekunywa mke wake.
Akalitoa shuka la Sonia akashusha suruali yake mpaka chini akapanda kitandani na kuipandisha ‘night dress’ ya Sonia juu,kwa kuwa hakuzoea kulala na kitu chochote ilikuwa rahisi kwa Mzee Urasa kufanya anachokifanya kirahisi.Mzee Urasa akafanya kama siku zote akiamini Sonia hana fahamu zozote zile,mpaka anamaliza mzunguko wake wa kwanza Sonia hakujigusa hata kidogo, aliogopa.Na alijua kuwa Mzee huyo ana bastola.Kujitingisha ama kufumbua macho yake kulimaanisha kuyaweka maisha yake matatani,bado alishindwa kuelewa wanaume wana matatizo gani.
Hiyo ilimfanya azidi kuwachukia zaidi,mbali na hapo alimuonea huruma Mzee Urasa,Ukimwi ulikuwa tayari damuni mwake.Baada ya dakika moja alihisi mwili wake unapanguswa vizuri,akafunikwa na shuka.Kitendo cha mlango kufungwa na Mzee Urasa kutoka chumbani kilimfanya aanze kulia machozi,alilia kwa uchungu na ndiyo siku hiyo alijuwa kuwa huo ndio ulikuwa mchezo wa Mzee huyo kila usiku!
“Eh Mu..ngu wangu”
Sonia alilia kwa kwikwi,mpaka asubuhi kunakucha.
***
Mzee Urasa alipigwa na butwaa la ajabu!Mpaka saa moja ya asubuhi mke wake hakutingishika kitandani,haikuwa kawaida hata siku moja.
Akamtingisha lakini wapi.
“Mama Happy”
Kilichompa Moyo ni mapigo ya mke wake yalikuwa yakidunda,hiyo ilimaanisha uhai upo.
“Mama Happy”Akazidi kuita!
Akavaa shati harakaharaka mpaka chumbani kwa Sonia na kugonga mlango,lakini hakuitikiwa.Akili yake ilimtuma wenda dawa alizoweka kwenye glass alikunywa mke wake,ni sawa alikuwa sahihi lakini hakuwa na uhakika ndiyo maana aligonga mlango wa Sonia.Kama ingekuwa hivyo sijui angeweka wapi uso wake.
***
Kilichomchelewesha Sonia kutoka chumbani ni funguo zake za gari,kumbukumbu zake zilimwambia kuwa aliziweka kabatini lakini hakuziona siku hiyo.Alivyofungua mlango wake akakumbana na Mzee Urasa.
“Shikamoo Baba”
Sonia aliamkia kwa wasiwasi,hapo ndipo Mzee Urasa alipata jibu lake.Kitendo cha Sonia kuzinduka mapema kilimuogopesha,alijua tayari siri yake imevuja ndiyo maana hata salamu ya Sonia aliitikia huku akiweka kichwa chake chini,alijisikia aibu na haya usoni.
“Mar..ahaba Mwanangu”
“Nilikuwa nataka kukuomba kitu?”
“Kitu gani?”
“Kuna pesa nimetumiwa,nahitaji kwenda kuzichukuwa kisha nirudi”
“Lini?lini Leo?”
Sonia hakutaka kuaga moja kwa moja,akili yake ilifanya kazi kwa kasi ya umeme.Ndiyo maana akadanganya angesema anaondoka siku hiyo angegundulika.
“Ndiyo Baba”
“Utarudi lakini?”
“Sina sehemu yoyote ya kwenda,lazima nitarudi tu”
“Basi wacha nikupeleke”
“Usijali,hata hivyo nitapitia kwa rafiki yangu mara moja”
“Hakuna shida,umesema utarudi eeh?”
“Nitaacha simu zangu,ni lazima nirudi”
“Sawa hakuna shida”
“Funguo zangu za gari sizioni,sijui zipo wapi”
“Oooh,Mama alizichukuwa juzi.Zipo chumbani kwangu”
Maswali aliyokuwa nayo kichwani Mzee Urasa hayakuwa na idadi kamili,bado alikuwa njiapanda haelewi lolote.Isingewezakana hata kidogo kwa Sonia kuamka muda kama huo kama dawa aliyoweka kwenye maji alikunywa.
“Itakuwa alikunywa au iliisha nguvu?Au alikunywa kidogo?”
Hayo ndiyo maswali yasiyokuwa na majibu yaliyokuwa yanapita ndani ya kichwa cha mzee huyu Urasa.Bado mke wake alikuwa nusu kaputi tena anakoroma,akachukuwa funguo na kutoka nazo Seblen ambapo alimkuta Sonia tayari keshajiandaa.
“Simu nimeziacha chumbani nitarudi muda sio mrefu”
“Sawa,gari yako nilikutengenezea”
“Shilingi nga…”
“Usijali”
Sonia aliondoka akiwa na hofu,akaingia mpaka ndani ya gari lake akiwa mwenye mashaka.Bado hakuamini kuwa anaondoka,akaingiza funguo ndani ya ‘switch’ na kuzungusha,gari ikawaka.Taratibu akalirudisha nyuma.Alivyohakikisha yupo tayari kwa kuondoka alikanyaga mafuta taratibu,kabla ya kufika getini moyo wake ukapiga kwa nguvu baada kuangalia kwenye ‘site mirror’ na kumuona Mzee Urasa analifuata gari lake akiwa na bastoa mkononi!

****
Mambo yaliyokuwa yanaendelea ndani ya Choo cha wanawake hayakuelezeka kiwepesi,watu walitaka kutumia vyoo lakini walivyotaka kuingia ndani ya mlango huo ulikuwa umepigwa ‘lock’ kwa ndani, kumaanisha kuwa kuna mtu anajisaidia.Hakuna mtu yoyote aliyeelewa kuwa ndani kuna mambo ya kishenzi yanaendelea.
Miguu ya Jemima ilikuwa imepanuliwa Leythan yupo chini yake, goti lake moja limegusa sakafu ulimi wake upo juu ya Mgodi wa Msichana huyu mrembo anaulamba,hakutofautishwa na paka alambae maziwa juu ya kisosi.Hicho ndicho kitu kilichokuwa kinaendelea ndani ya Club hiyo tena chooni.
Conie alikuwa kaunta anakunywa na kulewa hakuelewa lolote kuhusu Leythan kuwa yupo na mwanamke chooni.
Ndani ya club kulikuwa na watu wengi usiku huo wa Jumamosi kuamkia Jumapili.Conie alipapenda sababu ya uchangamfu uliokuwepo,kila nyimbo iliyokuwa inapigwa na Dj aliifurahia na kumkonga moyo.
Kazi yake ikawa ni kutingisha kichwa huku akiweka mikono yake hewani.Mawazo aliyokuwa nayo yote yalimwisha, kwa wakati huo alikuwa ana furaha iliyozidi kifani!
“Embu niwekee kinywaji changu,niende chooni.Ni wapi huku au kule?”
“Ni kule kwa juu,upande wako wa kushoto”
Conie alimkabidhi Muhudumu aliyekuwa kaunta glasi yake ya pombe na mzinga wa Konyagi.
Akatembea taratibu huku akitingisha kichwa na kupanda ngazi mbili na kuingia chooni,msongamano ulikuwa mkubwa watu walitoka na kuingia.Akapita choo cha katikati lakini mlango ulikuwa umefungwa kwa ndani,ilibidi aingie mlango unaofuata,akashusha sketi yake ya kimini na kuteremsha chupi chini,hapo ndipo alipokaa na kutoa haja ndogo.
“Ah shs aah aah aah Ib..ra aaah ivy..o ivyo”
Sauti ya puani iliyokuwa inatokea choo kinachofuata ilimfikia masikioni mwake,akasilikiza kwa makini.
Japokuwa mziki ulikuwa mkubwa na ulifika mpaka chooni lakini ya mwanamke akilalamika pia aliisikia vilevile.
Akatabasamu sababu kwa akili ya utu uzima aliyokuwa nayo alielewa kuwa kuna mwanamke mwenzake anashughulikiwa,haikuwa ajabu sana na hakutaka kujisumbua kuendelea, aliogopa kupandwa na midadi.
“Ah ah ah aaaaah aaaaah sssh aaaaah iv..yo ivy…o nishi.ke hapa”
Sauti ikazidi kusikika safari hii Conie alitulia ili ajue mwisho wake,sauti za puani zilizidi kuenea, ilielekea mtu anayepewa dozi hiyo alikuwa akikunwa kisawasawa! Kwa maana hiyo hakutaka kutoka mpaka ajue huyo ni mwanaume wa aina gani,sio kwamba alimtaka ili nayeye apewe hapana!
moyo wake ulihisi kumuona Mwanaume huyo ndiyo aridhike,akavumilia harufu ya choo kwa kama sekunde kumi na saba, ndipo aliposikia mlango unafunguliwa nayeye akatoka.
“Mkanda wako huo hapo chini”
Jemima alitoka na kumwambia Leythan aliyekuwa bado yupo ndani anapandisha suruali yake.Hapo ndipo Conie akajipitisha ili amuone mwanaume huyo.Moyo wake ukapiga mkambo, akahisi kama ameona vibaya akarudi kidogo nyuma.
“Ley…than”
Conie aliita baada ya kuhakikisha kweli ni Leythan.
Kwa jambo alilolishuhudia alidhani yupo ndotoni na muda mfupi atashtuka akute mambo ni tofauti,bado alikuwa ameganda kama barafu anamtizama Leythan aliyekuwa ndani chooni amepigwa na bumbuazi.Alijihisi amekuwa mdogo kama kifaranga cha kuku,hakuelewa ni kitu gani akiseme lilikuwa ni fumanizi lisilohitaji utetezi.
“Leyth..an”
Conie akaita tena safari hii machozi yalikuwa yakimlenga,alihisi moyo wake umechomwa na mkuki wenye moto.Jemima alikuwa kimnya anamtizama hakuelewa lolote lile.
“Kwani mbona sielewi,eti dada mb…”
“Nyamaza Malaya”
“Umeniambiaje?”
“Kama ulivyonisikia”
“Paaaaaa”
Sauti ya kibao kilisikika,Conie ndiye aliyepigwa ukofi wa shavu na Jemima.Hakuelewa kosa alilolifanya alivyorudisha kichwa nayeye akajibu kwa ukofi,hapo ndipo mambo yalipoanzia,wanawake hawa walianza kupigana misumbwi,
Wakisukumana huku na kule.
“Conie..Conie”
Jemima na Conie walikumbatiana wakivutana huku na kule,kazi ya Leythan ilikuwa ni kuwavuta na kusuluisha ugomvi.Ndani ya dakika moja wanawake walijazana bafuni.
“Conie,tuondoke”
Leythan alisema na kumvuta pembeni.
“Niache Leythan”
“Hapana siwezi”
“Nimekwambia niache”
Kuanzia hapo hakukuwa na maelewano mazuri kati ya Conie na Leythan.Mpaka wanafika wanapoishi Conie alikuwa akipiga kelele na kulia machozi.
“Usinishike,endelea na mambo yako”
“Conie nisikilize mpenzi wangu”
“Nikusikilize nini sasa?”
“Nikwambie kilichotokea”
“Uniambie nini Ley,Uniambie kitu gani.Hakuna haja ya kujitetea.Naomba uondoke tafadhali”
“Con…”
“Nadhani umenisikia,unakula kwangu.Nakulisha nakuvisha.Huna hata shukrani.Toka Leythan”
“Sasa nitaenda wapi usiku huu?”
“Kwa kahaba wako,toka kwangu”
Hakukuwa na punje ya utani kutoka kwa Conie kila alivyozidi kuongea ndipo hasira zilimpanda,akatembea mpaka kwenye kabati na kuanza kutoa nguo za Leythan. Na kuzitupa chini.
“Ondoka Leythan sikutanii”
“Lakini Coni..”
“Toka toka tafadhali”
Kitu alichokuwa anakisema ndicho alichokuwa anakifanya akatembea mpaka mlangoni na kuufungua, akatupa nguo za Leythan nje.
“Toka kwangu”
Kila alipojaribu kujitetea alishindwa,akajaribu kumshika lakini mkono wake ulitupwa mbali na kuambiwa atoke nje.Ulikuwa ni usiku mnene,Leythan hakujuwa ni wapi aende.Alijutia moyoni kwa jambo la kijinga alilofanya.Taratibu alitembea na kugeuka akidhani wenda Conie atasema ana mtania na arudi lakini haikuwa ivyo,macho ya Conie yalikuwa mekundu.
Kifua chake kilipanda juu ya kushuka,pua zake zikawa zinamchesha yote hiyo ni kwasababu ya hasira.Leythan alivyotoka nje akabamiza Mlango na kufunga na funguo,akajitupa kitandani na kuanza kulia kwa uchungu.
***

Hakuwa na ujanja mwingine wowote ule sababu hata geti lilikuwa limefungwa ndio maana akashindwa hata kuendelea kukanyaga mafuta ili atoe gari nje,akabaki anamtizama Mzee Urasa anayekuja akiwa na bastola mkononi mwake,moyo wake ukazidi kupiga kwa kasi mno.Akahisi mkojo unataka kumtoka.
“Kokoko”
Mzee Urasa akagonga kioo kwa nje.Sonia akajishauri kufungua.Akatafakari kwa kama sekunde tano kisha kubonyeza kidude maalum pembeni ya Mlango kioo kikashuka mpaka nusu.
“Kuna magazine yangu hapo kwenye dashbodi”
“Wapi?”
“Fungua hapo”
Sonia alikuwa akitetemeka na Swala hilo lilionekana wazi kwa Mzee Urasa.
“Oh samahani,kumbe nimekutisha”
Baada ya kuona ana bastola mkononi akairudisha kiunoni sababu aliamini ndiyo ilikuwa inamtisha Sonia.
“Ndio Baba”
“Pole sana,naomba hiyo Magazine.Ndiyo imenifanya nije mbiombio”
Sonia akaichukuwa na kumkabidhi Mzee Urasa magazine iliyojaa risasi ndani.
“Alafu mbona hujafungua geti,ngoja nikusaidie”
Bado hakuamini kama anaenda kutoka nje ya geti hilo akiwa salama ndiyo maana akashusha pumzi ndefu za ndani, Moyoni mwake alimshukuru Mungu huku kioo chake cha gari kikipanda juu,akalitoa gari getini alivyokata kona ya kwanza.Ndipo alipoongeza kasi huku akiangalia nyuma kama Mzee Urasa anamfuatilia.

Vitu vingi vilipita ndani ya kichwa chake.Hakuelewa ni nani alimkosea sababu majanga aliyopitia siku chache zilizopita tena mfululizo yalimuogopesha wakati mwingine alidhani wenda ni laana.
Licha ya hayo bado aliendelea kuamini kuwa ana maisha marefu ya kuishi duniani.
Aliendesha gari kwa makini mpaka alivyofika nyumbani kwake na kufunguliwa geti.
“Askari njoo”
Mlinzi mwenye mtutu akasogea karibu na bosi wake.
“Mtu yoyote akija kuniulizia mwambie sipo,umenielewa?”
“Ndio bosi”
“Ahsante”
Sonia akapandisha ngazi harakaharaka akanyoosha chumbani kwake.Hakufikiria kitu kingine zaidi ya kwenda kununua simu nyingine mpya,hakuwa na haja ya ku ‘renew’ laini sababu aliondoka nazo,Kwa Mzee Urasa aliacha simu bila laini.
Aliingia bafuni na kujimwagia maji,akatoka na kuvaa nguo nyingine.
“Duu nimekumbuka,wewe Suka,sukaaaa”
“Naam Bosi”
“Tyson yuko wapi?”
“Yupo chumbani kwake”
“Kamwite”
Nyumba ya Sonia ilikuwa kubwa na ndani yake kulikuwa na nyumba nyingine ndogo ambayo alilala Mlinzi wake,Tyson.
Siku hiyo hakutaka kutoka nje aliogopa kukamatwa na watu asiowajua.
“Kanikatie tiketi ya Precious Air ya leo jioni,na ninunulie na simu moja ya kawaida.Hata Nokia ya Tochi sawa tu”
Yalikuwa ni maagizo yaliyotoka kwa Sonia,Tyson alikuwa mbele yake anayasikiliza na kukabidhiwa pesa na funguo za gari.
“Alafu hiyo gari haina mafuta,utajaza ya elfu sitini”
“Sawa Bosi”
“Nakusubiri usichelewe sasa”
Tyson akatoka na kuingia ndani ya gari akimuacha Sonia anaingia seblen.
Hakufanya kitu kingine zaidi ya kuandaa baadhi ya nguo zake,habari za babu yake kuumwa zilimchanganya akili yake ilikuwa ni lazima siku hiyo apande ndege ya jioni aende Mkoani Kilimanjaro,Moshi.
***
Kwake aliamini ilikuwa kama bahati kupata tiketi ya ndege inayoondoka siku hiyo saa kumi na moja Jioni,kwa maana kuwa alibakisha masaa machache tu ili awepo uwanja wa ndege kwa ajili ya ukaguzi na safari yake ianze.
Wakati akijiandaa simu yake mpya ilikuwa kwenye chaji.Akaweka kila kitu sawa kabisa ndani ya begi,nguo chache ndizo alizobeba.
Baada ya hapo alimuita Tyson ili aandae mazingira ya kumpeleka uwanja wa ndege.
Na ndipo hapo alipopata nafasi ya kumpigia simu Dustan akimueleza mchakato mzima wa safari yake.
“Nitakuwa KIA,nitakusubiri”
“Sawa Anco!”
Alivyokata simu akamgeukia Tyson.
“Ninasafiri leo,nipeleke Airport alafu utarudisha gari”
“Okay”
Hakuwa na begi kubwa la kutisha,akatoka nje na kuingia viti vya nyuma.Safari ya kwenda Uwanja wa ndege ikaanza mara moja.
***
Sonia alifika uwanja wa ndege akiwa amebakisha dakika sitini na saba ili ndege itoboe mawingu kwa maana hiyo aliwahi na alikuwa ana muda mwingi wa kujivuta lakini hakutaka kufanya hivyo ndiyo maana alivyofika tu,alishuka na kutafuta mlango wa kuingilia.
Baada ya kufanyiwa ukaguza akatafuta namba ya geti walipokuwa wasafiri wenzake.

Kichwani kwake kulijaa mawazo chungu mzima.Aliwaza vitu vingi sana hususani maisha yake kwa ujumla,hakuelewa muafaka,japokuwa alielewa binadamu ni lazima aonje umauti.Alivyokumbuka ugonjwa wake ndipo alipokosa raha kabisa.
“Dada,nadhani unaondoka na Preciuos air namba 138k?”
Mrembo aliyevalia sketi ya kijani na shati jeupe la mikono mirefu alimuuliza Sonia.Baada ya kumuona yupo peke yake, wenzake wote wamemuacha na alivyoangalia tiketi yake,akashtuka na kumuangalia muhudumu wa ndege.
“Ndio”
“Wenzako washaingia kwenye basi”
“Samahani sikujua na pia ahsante”
“Uko sawa?”
“Niko sawa ndio usijali”
Sonia akavuta begi lake na kuliweka mkononi na kuteremsha ngazi,ambapo alikuta basi kubwa lililobeba wasafri wenzake akaingia na ndipo lilipoanza safari.
Ilielekea ni yeye ndiye walikuwa wanamsubiri,Uwanja ulijaa ndege nyingi na basi kubwa likasimama umbali wa mita tano kutoka shirika la ndege ya Precious air,abiria wakashuka akiwemo Sonia.Akapanda ngazi taratibu na kuingia mpaka ndani, kazi yake ikawa kutafuta siti yake,alivyoipata alikaa na kushusha pumzi ndefu akisubiri maelekezo mengine ya ziada.
*****
Haikuwa safari ndefu kwake,ndani ya dakika kama hamsini kipaza sauti kilisikika kuwa wanakaribia kutua mkoani Kilimanjaro, hivyo abiria wote walitakiwa kufunga mikanda yao kwa ajili ya usalama,hicho ndicho kilichotokea.Kichwa cha ndege kikaanza kutizama chini na matairi yakaanza kuchomoza.Ilivyotua ilitikisika kidogo na kukaa sawa hapo ilikwenda kwa kasi ya risasi na taratibu kupunguza mwendokasi na kusimama kabisa kwenye maegesho maalum.
“Dada samahani”
Sauti ya kiume ilimshtua Sonia aliyekuwa amesimama anatoa begi juu.
“Bila samahani,nikusaidie nini?”
“Sijui nakufananisha”
“Na nani?”
“Na mwanamke Fulani hivi alikuwa na mahusiano na mcheza mpira,Partson Ngogo”
“Hapana sio mimi”
“Dada”
“Nimekwambia sio mimi”
Maongezi hayo yalimtia kinyaa,akachefukwa. Katika maisha yake hakutaka kumsikia Partson hata siku moja hata hivyo alikuwa teyari amemsahau ndiyo maana alisonya na kuweka vizuri begi lake dogo mkononi na kutembea kuelekea mlangoni.
Magari maalum ya kuweka ngazi yalikuwa teyari mlangoni abiria wakaanza kushuka,kwa kuwa hakuwa na mzigo mwingine wowote ule alipitiliza mpaka mlango wa kutokea abiria.
“Soniaaaa,Soniaaa”
Sauti hiyo ilimshtua,hakuwa na haja ya kuuliza sababu aliijua ilikuwa ya Dustan.Ni kweli alivyogeuka alimuona pembeni amevaa suti nyeusi.
“Shikamoo Anco”
“Marahaba pole na safari”
“Ahsante nishapoa”
Karibia robo tatu ya wanaume waliokuwa wanapishana na Sonia hawakuwa na uvumilivu walilazimika kugeuza shingo zao bila kupenda,Sonia alitisha kwa uzuri, japokuwa alivaa suruali ya ‘Jeans’ lakini umbo lake lilitokeza nyuma akawa tatizo, kiuno chake kilichobinuka kiliwapa watu shida,Usoni ndiyo usiseme.
“Babu anaendeleaje?”
“Ana hali mbaya sana,si unajua uzee tena”
“Poleni sana”
“Tushapoa,anahitaji kukuona”
“Jamani,ndiyo tunaenda sasa hivi?”
Maongezi hayo yalifanyika huku wakiwa wanatembea kuelekea kwenye maegesho ya magari,gari la Dustan lilikuwa limeachwa milango wazi kumaanisha kuwa kuna mtu ndani anawasubiri.
“Sonia huyu pia sijui utamuita anco ni mtoto wa Stanley Shayo, mdogo wake na Babu yako”
Dustan alianza utambulisho baada ya kufika ndani ya gari.
“Ahsante kwa kukufahamu shikamoo Anco”
Sonia akasalimia lakini salamu haikuitikiwa.
“Shikamoo Anco”
Akarudia tena.
“Oh,Marahaba hujambo?”
Godson akatoa mkono ili kusalimiana na Sonia,uzuri wa ndugu yake huyu ulimtibua akili ndiyo maana akamtekenya mkononi.
“Tueshimiane basi”
Hilo ndilo neno alilosema Sonia kwa ukali huku akitoa mkono wake,Godson akahisi aibu ajabu!
“Usinichukulie hivyo unavyodhani,jaribu kujiheshimu”
Sonia aliendelea kupigilia msumari kauli yake,Dustan aliyekuwa nyuma ya usukani alishindwa kuelewa ni kitu gani kimetokea.
“Sonia vipi tena?”
“Anco….”
Sonia alitaka kuongea lakini akasita,Utu uzima na busara alizokuwa nazo Dustan alielewa nini kiliendelea.
“Godson,huyo ni ndugu yako!”Alisema na kuwasha gari.
Gari likageuzwa na safari ya kwenda K.C.M.C ikaanza mara moja,Sonia hakutaka kupumzika alitaka kumuona Babu yake hospitalini.
Haikuchukuwa muda mrefu wakawa wamepaki gari hospitali hiyo kubwa ya K.C.M.C wote wakashuka,muda wote Godson alijisikia aibu na haya usoni.
Sonia hakuwa na habari naye wakatembea mpaka mapokezi.
Kitu kilichomshtua Sonia ni baada ya kumuona mtu anayemfananisha japokuwa hakuwa na uhakika sana,alizidi kumtizama mwanaume huyo aliyekuwa amekaa juu ya benchi.
“Sonia”
“Mustapha,unafanya nini hapa?”
Sonia nayeye akauliza kwa mshangao,baada ya kupata uhakika.
“Kumbe mnafahamiana?”
Dustan nayeye akatia neno,alionekana kushangazwa.
“Yeah namfahamu huyu”
“Basi ni shemeji yako”
“Kivipi?”
“Huyu mchumba wa Dada yako, Nasra”
Sonia alimtizama Dustan mara mbilimbili,hakuelewa sentensi hiyo ina maana gani.Hapohapo mlango ukafunguliwa Nasra akatokeza.
“Baba mdogo Dustan,kumbe usharudi?!”
Kauli hiyo ndiyo ilizidi kumfanya Sonia ashindwe kuelewa vizuri,imekuaje Dustan na Nasra wamejuana,akawa njiapanda.
“Haaa Sonia,umefuata nini hapa?za siku nyingi?”
Kila mtu alikuwa na kiulizo na mwenye maswali kichwani kwake.Sonia ndiye aliyeonesha mshangao wa waziwazi.
Kabla ya kuendelea kuulizana mengine wote wakatizama kulia kwao,Rukia na Mwanamke Mzee wakatokeza.
“Wajukuuu zangu”
Hivyo ndivyo bibi huyo alivyosema kwa mshtuko!Maneno hayo ndiyo yakazidi kuwachanganya zaidi wanawake hawa warembo, Sonia na Nasra!



Historia ya Sonia kama ingeandikiwa kitabu na watunzi nguli maarufu nchini Tanzania kama Eddazaria G.Msulwa ama Hussein O. Molito basi kwa siku wangeuza nakala mia tisa.Historia ya Sonia iliwafanya watu wadondoshe machozi waliokuwa wanamsikiliza, hata baadhi ya manesi waliokuwa pembeni wanapita wengine walidiriki kusimama na kumsikiliza mwanamke huyu mdogo aliyepita kwenye shida nyingi.Sonia alieleza kila kitu tangu alivyokuwa nchini Sweden,alivyofika kwenye kiti cha umeme alichokalishwa ndipo alipomwaga machozi zaidi.Historia yake haikuishia hapo,aliisogeza mpaka siku chache alivyotaka kuuwawa msituni madale ndipo akakutana na Nasra,lakini jambo moja ambalo hakulielezea ni kuhusu tatizo la kuwa na ugonjwa wa Ukimwi,aliogopa!
Ugonjwa wa Ukimwi ulichukuliwa ni wa kihuni,aliogopa kutengwa na kuchukuliwa Malaya kama jamii ilivyoutafsiri ugonjwa huo.Bibi yake muda wote alikuwa akimwaga machozi,Nasra ndio usiseme.Dustan machozi yalimlenga ndiyo maana akaamua kusogea kando na kutoa leso yake na kupangusa machozi,kila mtu alisahau kuwa ana mgonjwa.Kila mtu alimsikiliza Sonia,hawakutofautishwa na watu wanaosikiliza redio.
Sonia alihitimisha na kukumbatiwa na dada yake Nasra,kila mtu alimtizama Dustan sababu ndiye aliyempigania nchini Sweden.
“Dustan”
Mustapha ndiye aliyeita na kumuendea,akamshika bega. Dustan akageuka machozi yalikuwa tayari yanamtoka.Moyo wake ulimuuma.
“Kila kitu kipo sawa,Wewe ni mwanaume jasiri sana”
Captain Mustapha akatoa pongezi zake na kumpa mkono.
“Ahsante sana,Mgonjwa anaendeleaje?”
Haraka akabadili mazungumzo ili asiendelee na majonzi,alimtizama Sonia aliyekuwa anabembelezwa na Nasra.
“Sonia”
“A…be Anco”
“Usilie,futa machozi.Yote yashapita haina haja ya kukumbuka.Upo salama sasa hivi.Mshukuru Mungu”
“Ah..sante Anco”
Hata baada ya kubembelezwa Sonia aliendelea kulia kwa kwikwi tu.Upande wa pili wa shilingi alifurahi kumjua dada yake ndiyo maana akazidi kumkumbatia,ndugu walikuwa teyari wamejuana.Bibi ndiye alitoa siri hiyo.

Rukia alifurahi sana japokuwa alishangazwa na Sonia jinsi alivyokuwa mtu mzima,sababu ndiye yeye aliyemlea kipindi cha marehemu Nickson.
“Nah..itaji kumuona B..”
Kabla ya Sonia kumalizia sentensi yake.Daktari akatoka chumba alichokuwa Mzee Shayo,kila mtu akamtupia macho, kupitia uso wa daktari huyo kuna kitu walikisoma.Hakukuwa na matokeo mazuri ndiyo maana kila mtu ndani ya moyo wake aliomba jambo hilo lisiwe la kweli.
“Dokta Vipi?”
Dustan akajikaza kisabuni,japokuwa aliongea kwa unyonge sana.
“Embu njoo kidogo ofisini kwangu”
Kauli hiyo ndiyo ikamfanya mke wa Mzee Shayo Bibi Mackleshi,alie kwa sauti sababu alishajipa jibu moja kwa moja kuwa Mume wake ataaga dunia ingawa hakuwa na uhakika asilimia mia moja.
“Dustan”
Dokta alianza mazungumzo na kutoa miwani yake,baada ya kufika ofisini.
“Naam Dokta”
“Mzee anaumwa sana,na pia uzee unachangia.Sitaki jambo ambalo sote hatutaki litokee.Kwa maana nachokushauri asafirishwe mpaka India.Kama mpo tayari tuanze mipango”
Dustan akashusha pumzi ndefu.
“Unao muda wa kujifikiria Mr.Dustan”
“Okay sawa”
Akatoka nje akiwa mnyonge hali hiyo ndiyo ikawachanganya watu kabisa.
“Uwiiii Mume waaaaanguuuuuuu,kwanini umeniacha mapema kiasi hichi,yewomiiii.Mungu weeeee”
Bibi Macklesh alianza kulia na kudondoka chini kila mtu akamgeukia,Sonia ndiyo akaangua kilio kikubwa,Nasra ndio kabisa.Dustan akapigwa na butwaa la ajabu akashindwa ni kitu gani akifanye.
“Jamani,Msilie Mzee ni Mzima”
Kila mtu akamgeukia.
“Imekuje?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Mustapha.
“Dokta ame…kwa..mbiaje?”
Hapohapo Sonia akaibua swali lingine.
“Baba md..go Dustan.Tua..mbie ukweli”
Nasra nayeye akauliza.
Dustan alitupiwa maswali mengi,hakuelewa aanze kumjibu nani.Akabaki njia panda.Kelele za kilio zilienea kordo nzima,ikamfanya daktari atoke ofisini kwake.Hiyo ikamlazimu aeleze kila kitu kilichotokea.
“Mimi nipo tayari kutoa pesa,ni kiasi gani?”
Sonia ndiye aliyeongea na kusimama kwa ujasiri.Kila mtu akamgeukia na kumuangalia mwanamke huyu,hata Nasra alipigwa na bumbuazi.Pesa alizotaka kutoa Sonia ili kumsafirisha babu yao zilikuwa nyingi,kwa hesabu zake za harakaharaka ulikuwa ni kama mshahara wake wa mwaka mzima,ndiyo maana akashindwa kumuelewa Sonia.
“Ni kiasi gani daktari?”
Sonia akauliza tena swali.
“Upo tayari kutoa?”
“Ndio”
“Basi njoo ofisini kwangu”
Dustan nayeye akamfuata nyuma wote wakaingia ofisini kwa daktari,bili ikaletwa mara moja.Ilikuwa ni shilingi milioni sitini za kitanzania kuanzia tiketi mpaka upasuaji wa Mzee Shayo na kuwekewa figo na Mifupa yake kufanyiwa matibabu.
“sawa nitatoa”
“Mimi nitachangia pia”
“Acha Anco Dustan,mimi nitagharamia.Usijali”
Dokta alishangazwa sana,pesa zilikuwa nyingi mno kutolewa na mtu mmoja tena mwanamke mdogo kama Sonia.Bila kuongea chochote akatoka nje na kutoa simu,akaonekana kama anatafuta namba fulani kwenye orodha ya majina.Baada ya kuzipata aliipa simu ‘ok’
“Hallooo Victor”
“Naam Sonia”
“Habari za wakati huu?”
“Nzuri tu,za kupotea?”
“Sio mbaya,sasa nina shida hapa.Upo ofisini?”
“Hapana,sasa hivi ni usiku”
“samahani, ninahitaji kudraw pesa kesho.Nitakuja basi”
“Upo wapi?”
“Nipo Moshi”
“Haina haja ya kuja,CRDB pia tuna tawi letu huko Marangu.Ngoja nikuunganishe na mtu mmoja hivi.Nakutumia namba zake sasa hivi”
“Nashukuru Victor”
Sonia akakata simu.Kila mtu alivyopewa habari za Sonia juu ya kuyaokoa maisha ya babu yake walishindwa kuelewa,kila mtu alimtolea macho.Bibi yake alimshukuru na Kumpa Baraka zote.
“Bibi usijali,ngoja nifanye mazungumzo na watu kwa ajili ya hizo pesa ikiwezekana kesho asubuhi awe keshapelekwa India”
Kila kitu kilichotokea kilikuwa ni kama maigizo,Kuanzia Muda huo Sonia alikuwa na Simu sikioni tu,akitembea huku na kule alitaka kupakuwa pesa hizo nyingi kutoka benki tiketi zikatwe na viza ipatikane.
***
Hekaheka za kutafuta Viza zilianza mara moja sababu pesa ilipatikana,Mzee Shayo akawekwa katika mazingira ya kusafiri.Dokta Khan kutoka India,Jijini Mombai,ndiye alikuwa akifanya mawasiliano na ubalozi wa India, haikuwa kazi ngumu sababu viza ilitakiwa mara moja ndiyo maana baada ya siku mbili ikawa tayari zimepatikana.
“Nasra,utaenda na Babu.Mimi nitabaki”
Moyo wa Nasra ulipiga kwa nguvu,alivyoambiwa kuhusu safari.
Katika maisha yake hakuwahi kupanda ndege wala kutoka nje ya nchi.Fursa hiyo kwake ikawa kama kuokota kipande cha almasi shambani.
“Sawa dada hakuna shida”
Tiketi ya Dustan,Nasra pamoja na Mzee Shayo zikawa tayari na safari ndiyo ilikuwa inasubiriwa tu.Mzee Shayo hakuweza kuzungumza kitu chochote maradhi ya figo yalimsumbua na mifupa.Usiku wa saa moja siku ya Alhamis kilisikika king’ora cha gari la wagonjwa mahututi.
Mzee Shayo akawekwa juu ya machela,ikaanza kusukumizwa mpaka ndani ya gari.
“Sonia utaweza kurudisha gari yangu Dar es salaam?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Dustan wakiwa ndani ya gari,mbele yao kuna ‘Ambulance’ inakimbia kuwahi uwanja wa ndege KIA.Ndege ya shirika la INDIA AIRWAYS ilikuwa inatarajia kuondoka saa sita ya usiku.
“Hapana Anco,labda niongee na Shemeji Mustapha”
“Sawa,sababu sitokaa sana India.Inanibidi nirudi kuna kazi natakiwa kumalizia Dar”
Mikono ya Dustan ilikuwa juu ya usukani anaendesha gari kama mwendawazimu,hakutaka gari la hospitali limuache ndio maana akawasha ‘hazard’kumaanisha kuwa ana dharura.
Hawakuchukuwa muda mfupi wakawa wameingia uwanja wa K.I.A.
Wauguzi watokeza mara moja,ilionekana walijua ujio wa mgonjwa huyo.Machela ikashushwa harakaharaka ikaanza kukimbizwa kupitia mlango maalumu.
“Nasra”
“Abee Sonia”
“Safari njema,mimi nitabaki nyumbani na bibi kwanza”
“Ahsante dada angu ubaki salama,Mustapha akirudi kutoka Arusha uniagie sababu naona simpati simuni”
“Usijali kuwa makini,uwe unanijulisha kila kinachoendelea”
“Sawa”
Baada ya kuagana na Nasra akamgeukia Dustan,wakapeana mikono hapo ndipo walipoachana.
Sonia hakutaka kubanduka uwanjani mpaka aliposhuhudia ndege ipo angani,akapunga mkono na kuwaaga.Japokuwa aliamini haonekani lakini alifanya hivyo.

****
“Baba,nina amini huko ulipo unanisikia.Umeniacha nikiwa bado nahitaji penzi lako Baba yangu.Nitakukumbuka daima”
Ilikuwa ni asubuhi sana ya saa kumi na mbili,baridi lilikuwa linapuliza na kuingia mpaka ndani ya mifupa.Lakini Sonia hakusikia alikuwa katikati ya shamba la migomba nyuma ya nyumba yao,mbele ya kaburi la Baba yake Marehemu Nickson Shayo.Aliongea maneno ya kutia huruma huku akitizama Msalaba uliokuwa umeandikwa jina la baba yake siku aliyozaliwa na kufariki.
Kama ungemuona ungedondosha machozi na kulia,Sonia alitia huruma sana.
“Mama,nina amini pia huko ulipo unaniona.Nina amini ipo siku tutaungana sote na kuwa wenye furaha.Naw…penda sa..na wazazi wa..ngu.Kama ningekuwa na uwe…zo wa kurudisha siku nyuma..Ning..fanya hi..”
Kwikwi ilimba-na akashindwa kumalizia maneno aliyokuwa anataka kuongea,ghafla akahisi ameshikwa bega.
“Soniaa Mwanangu,usilie”
Ilikuwa ni sauti iliyomzidisha machungu sana,Rukia nayeye alifika eneo hilo.Hata yeye alilengwa na machozi alivyomkumbuka Nickson,siku hiyo ilikuwa ni siku ya huzuni sana.Wakawa wanalia tu.
Kitu kilichowakatisha ni baada ya kuhisi kama mtingishiko,wakatulia kidogo,upepo ulianza kuvuma taratibu hapohapo ukachanganya vumbi likaanza kutimka,wakashindwa kuelewa ni kitu gani kinatokea.
“So..niaa so..so..so..so..ni..aaaaa”
Sauti hiyo ya mwangwi ndiyo ikazidi kuwachanganya akili.Kila mtu akataka kutafuta njia ya kukimbia lakini ilishindikana kutokana na vumbi kuwa jingi.
“Sooo…soso…sosoni Mwaaaaanangu,usiogooope”
Wote walitandwa na hofu,mapigo yao yakapiga kwa kasi.Walivyogeuka nyuma yao waliwaona watu wawili wamevaa mashuka meupe.Kwa haraka sonia aliwatambua, alikuwa ni Baba yake na Mama yake Mzazi.Mara ghafla wakapotea.
“Soniaaaa mwanangu”
Sauti hiyo ikajirudia tena,alivyogeuka nyuma akawaona wametokea juu ya kaburi.Wote wakazidi kutetemeka kwa hofu.Ardhi ikazidi kutingishika,wakadondoka chini.
Ghafla Sonia akavutwa na kukabwa na Baba yake mzazi shingoni.
****
“Shindwaaaaaaaaa!”
Sonia alikurupuka kutoka usingizini ghafla,akasimama mpaka ukutani na kuwasha taa kwa uwoga,ndoto aliyokuwa anaota ilimtisha kupita kiasi,japokuwa kulikuwa kuna baridi lakini jasho lilimtoka sio kawaida.Mpaka kunakucha hakupata usingizi,akashindwa kuelewa ndoto hiyo ina maana gani.


*******
ENDELEA KUSOMA HADITHI NA SIMULIZI ZA MTUNZI….EMMANUEL F.KWAY(THE STORY MASTER)

0 comments:

Post a Comment

BLOG