Search This Blog

Sunday, May 31, 2020

SLAVE SEX SEHEMU YA 8/10


SLAVE SEX
MTUNZI….EMMANUEL F.KWAY(THE STORY MASTER)
AGE…(18+)
WatsApp…+255718 862176
SEHEMU YA 8 KATI YA 10
*******

“Mama,nimefurahi kumjua Brenda.Amekuwa sana nakumbuka nilikuwa nam-beba,leo keshakuwa
mdada”
“Ni kweli mwanangu Sonia,hata wewe umekuwa sana khaaa..umenenepa mno”
Kila mtu alikuwa amechangamka kupita kiasi,ndani ya moyo wa Sonia alikuwa na mengi sana ya kuongea na Brenda ili amuwahi,hakutaka mdogo wake apate maambukizi ya ukimwi hakuwa na uhakika kama jambo alilokuwa anataka kulifanya aliwahi au amechelewa ingawa alitaka kujaribu.
Brenda na Sonia siku hiyo waliongea kama hawakuwahi kukutana na kupashana masaa machache kabla.
“Mama”
Brenda akaita.
“Abee”
“Naomba leo nikalale kwa dada Sonia”
“Ni sawa tu,huyo ni ndugu yako,ondoa shaka”
“Ahsante Mama”
Pombe ziliendelea kunyweka.Sonia na Brenda wakaamua kuondoka zao ilivyofika usiku wa saa nane.
****
“Ndi..o hiv..yo mdooogo wa…ngu.Tafadhali na..omba uachane na Sebasti….n.Hayo ndiyo maneno nay..okwambia.Nina uhakika ana uk..miwi”
Hakuwa na sababu ya kuweka jambo hilo ndani ya kifua chake,alimuhadithia kila kitu mdogo wake huku akiwa analia machozi ya kwikwi.
Historia yake ilikuwa ya kusisimua kuliko kawaida, Brenda akajikuta analia na kumfuta dada yake machozi,wote wakakumbatiana.
“Pole dada Sonia,hayo yote ni maisha”
Siku hiyo asubuhi hawakunywa chai,kila mtu alikuwa akilia machozi,kulikuwa ni kama kuna msiba nyumbani hapo.
***
“HAIWEZEKANI,ETI ANA UKIMWI.MUONGO TU BONGO NI USANIII,HANA UKIMWI YULE ANATAKA NIMUACHE SEBA KIRAHISI ILI YEYE AFAIDI,HAPANA MIMI NA SEBA MPAKA KIFO NA LAZIMA NIMWAMBIE SEBA KUWA YEYE NDIYE SONIA.HAPANA KWA KWELI HATA MIMI DADA YANGU ANANIFANYIA MAIGIZO?HAHAHA KWELI DUNIA IMEKWISHA”
Brenda alikuwa akiwaza kichwani mwake,siku ya tatu baada ya kuongea na Sonia.Maneno aliyoambiwa hayakumwingia akilini hata kidogo,haikuwezekana hata kidogo kuamini kuwa dada yake Sonia ana virusi vya ukimwi,jinsi alivyonenepa na mwenye afya isingekuwa rahisi kukubali.Bado alimpenda Sebastian na alijua zile ni njama tu za kuachanishwa naye.
Bahati nzuri kwake, siku hiyo alipata wazo hilo akiwa hotelini,akakurukupa kama mgambo,akashuka kitandani akatembea mpaka mlangoni kwa Sebastian na kuanza kugonga mlango,ilikuwa ni lazima amwambie Sebastian ni wapi Sonia alipo.
“Who is knoking?”
Sauti ya Sebastian ilisikika akiwa ndani chumbani,kwa ndani ikasikika sauti ya kike.Brenda akazidi kupagawa.
“It's me Brenda”(Ni mimi Brenda)
“It still Morning,what’s up!”
“Please we have to talk,it’s important”(Inabidi tuzungumze,ni muhimu)
“Okay”
Brenda akatulia mlangoni,kwa mbali alihisi Sebastian anazungumza na mtu tena ilikuwa ni sauti ya kike.Moyo wake ukazidi kumuuma.
Dakika moja baadaye mlango ukafunguliwa Sebastian akatoa kichwa nje,kiwiliwili akakiacha ndani.
“Jazz!”(Sema)
“I have seen Sonia”
“Whaaaaaat?”(Nini)
Sebastian akauliza kwa hamaki huku akimtizama Brenda machoni,hakuwa na uhakika kama alisikia vizuri.
“Please,come again!”(Tafadhali,rudia tena)

 Maneno aliyokuwa anayasikia kutoka kwa Brenda bado aliendelea kuyatafsiri ndani ya akili yake,ndiyo maana alikuwa ameganda anamtizama.
“Sonia yupi unayemsemea wewe?”
“Sonia,ambaye aliwahi kuwa mpenzi wako,mkaachana kisa Mama yake alikuwa ni muathirika wa Ukimwi”
“Mwongo umemjuaje?”
Sebastian alikataa na kugeuza shingo yake akitaka kuingia ndani,kabla hajafunga mlango, akashikwa mkono.
“Wewe na Baba yako mlitaka kumuuwa,mkamtesa na kumuweka kwenye kiti cha moto nchini Sweden”
Kitu hicho ndicho kikambutusha Sebastian,katika kumbukumbu zake hakuwahi kumuambia Brenda lolote juu ya historia yake na Sonia.Hicho ndicho kikamfanya amuangalie Brenda machoni huku akimdadisi.
“Umesemaje?”
“Sonia namfahamu,Sonia Shayo alikuwa anasoma Stockholm University”
“Ulimjuaje wewe?”
“Unaona sasa,vaa nguo nikupeleke kwake”
“Kweli?”
“Ndiyo”
Hakukuwa na sababu nyingine ya kusubiri,Sura ya Sonia ilimjia kichwani akili yake ikavurugika,akatembea mpaka kabatini na kuvuta ‘jeans’
“Sebastian vipi?”
Ilikuwa ni sauti ya msichana aliyekuwa naye chumbani.
“Nisubiri,nakuja sasa hivi”
Kwa namna alivyokuwa anavaa 'Jeans' hakutofautishwa na mtu anayeunguliwa na nyumba.Muda wa kuvaa shati hakuwa nao akatoka hivyohivyo nje, shati mkononi.
“Brenda,Brendaaa.Twende basi”
“Nakuja namalizia kuvaa”
Jinsi Sebastian alivyotembea iliogopesha, alitembea kwa hasira na harakaharaka kama mwanajeshi aliyepoteza mtutu.Hakuelewa ni kitu gani amfanye Sonia endapo akikutana naye hana kwa hana.
“Ingia ndani ya gari”
“Lipi, hili?”
“Ingia ndani ya gari bwana”
Sebastian alitetemeka kwa hasira,akaongea kwa sauti ya juu mno.
***
Pombe alizokunywa usiku wa jana yake Club zilimchosha akiwa bado kitandani asubuhi,alihisi kichwa chake kinamuuma kwa mbali,alielewa kabisa hiyo ilikuwa ni ‘hangover’ hivyo haikumpa shida alichofanya ni kuweka shuka kando na kutembea mpaka seblen akafungua friji na kutoa maji ya baridi.
“Ngoja nichemshe supu ya kuku,hii hangover sio ya kawaida”
Sonia akajisemesha mwenyewe,akaingia jikoni na kuwasha jiko la gesi,akafanya kila anachojua yeye na kutembea mpaka seblen.Hakukaa sawa akahisi mlango wake unagongwa.
“Naniiiii?”
“Mimi Brenda,dada Sonia fungua”
“Sawa nakuja”
Hakuwa na wasiwasi wowote,akiwa na kanga moja peke yake, akatembea mpaka mlangoni na kufungua.Butwaa alilopigwa halikuwa na kipimo chake,mbele yake alikuwa amesimama Sebastian,macho yake yakiwa mekundu.
“Sebasti..paaaa”
Sonia alipigwa kibao kikali akaingia nacho ndani, kinyumenyume.
***
“Ah kaka,ndiyo hivyo sasa hivi ningekuwa sina inshu,ningekuwa nyoka wa kibisa.Mimi nakupa hiyo siri wewe mwenyewe, mimi naondoka naenda kuishi Mombasa na yule dogo anakuja”
“Ndugu yangu una Mungu,mshukuru Mungu sana”
“Nichonge sasa kwa nyuma hapa kidogo,pitisha pitisha mashine na huku”
Historia ya Leythan jinsi alivyonusurika kufanyiwa unyama na Mzee Ikanza, ilikuwa ya kusisimua mno,mpaka siku hiyo hakuamini kama amepona na mwiko wake upo salama salmin!aliendelea kuamini kuwa kitu kilichokuwa kimetokea kilikuwa ni ndoto tu,mtu mmoja aliyemuamini katika maisha yake ni Jumanne,kinyozi wake wa nywele.Ukihitaji siri ya Leythan basi ukimuona Jumanne lazima ungepewa mkanda wote.
“Kwahiyo sasa,unaacha mambo yako?”
“Mambo gani?”
“Ya wanawake”
“Embu ninyoe mzee”
Bahati mbaya Leythan akajitingisha mashine ikamkata, damu zikaanza kumtoka na kuchuluzika usoni.
“Haa mwanangu,umenikata?”
“Bahati mbaya,ngoja nikufute”
Hicho ndicho kitu kilichotokea.
Hawakukaa dakika mbili watu wawili wakaingia wamevaa suti, kwa harakaharaka alikuwa ni bwana harusi na mpambe wake na walionekana walikuwa na haraka mno.
“Bro nina haraka,nichonge fasta fasta.Nina dakika thelathini tu”
“Poa kaa”
Bila mashine kufanyiwa kitu kingine chochote ama kupashwa moto,Bwana harusi akakaa kitini akidai ana haraka mno.Mashine ikapita kichwani,bahati mbaya ikamchubua nayeye,tayari alipata ukimwi bila kujijua,Kwa njia ya kutumia kitu chenye ncha kali Bwana harusi akawa ameingiza kirusi cha ukimwi ndani ya damu yake,Leythan ndiye alikuwa chanzo.
Alivyomaliza kunyolewa akajifuta damu zilizokuwa kichwani,akatoka haraka na mpambe wake, akiendelea kudai kuwa amechelewa kanisani.
**
Kufumba na kufumbua alihisi amelowana,zilikuwa ni damu nyingi mno.Conie alizidi kutetemeka alimshuhudia mume wake anakata roho,sime aliyokuwa ameishika aliidondokea ikatumbukia tumboni mwake.Mzee Ikanza alikuwa akitafuta pumzi kwa shida anaweweseka.Conie alizidi kuchanganyikiwa, mambo kwake yalikuwa yameharibika,mlinzi wa Mzee Ikanza alilishuhudia tukio zima, akabaki ameganda anaogopa sababu Conie alikuwa ana bastola mkononi mwake,alihofia uhai wake ndiyo maana akahisi miguu yake imepigwa ganzi.
“Tulia hiv.yo hivyo”
Conie aliongea kwa Uwoga,bastola ikiwa mkononi mwake amemlenga mlinzi.Uwezo wa kufyatua hakuwa nao,aliogopa kuuwa japokuwa alikuwa tayari ana kesi ya kujibu.Alishika bastola huku akiwa anatetemeka kama mwenye kifafa.
“Sogea huku,leta funguo za gari upesi”
Hakujua ni muda gani funguo alizitoa,akamtupia Conie.
“Sogea huku”
Hizo ndizo kauli alizotoa mwanamke huyu Conie huku akiwa katika hali hiyo ya uwoga usiku huo.
“Geukia kule”
“Taf..fadhali,mi..mi sitosema”
“Nyamaza”
Ujasiri aliokuwa nao hakuelewa umetoka wapi,akaokota gongo na kumpiga nalo kichwani mlinzi,alivyohakikisha amedondoka, haraka akaingia ndani ya gari.Jinsi alivyolitoa ilitisha.Kichwa chake hakikuwa sawasawa, alikuwa kama mwendawazimu,mwilini alijaa damu.
“Leyth…an Leyth..an”
Conie aliendesha gari akiwa kwenye hali ya kuchanganyikiwa,hakuelewa anapoelekea.Lakini alipiga macho yake huku na kule,akimtafuta Leythan.
“Leyt..an Leyt..han upo wapi ja..mani”
Akazidi kuangalia huku na kule,ghafla akaona kama kivuli cha mtu.Alivyoangalia vizuri akagundua kuwa ni Leythan,akaweka gari pembeni.
“Leythan,usikumbie ni mimi.Leythaaaan”
Hali ya uwoga bado alikuwa nayo ndiyo maana alikuwa anakimbia,alijua tayari Mzee Ikanza amefika na yupo ndani ya gari.
“Conie”
“Njoo tafadhali”
“Mbonaa,hivyooo?”
“Sijui,ingia ndani ya gari”
Damu alizokuwa nazo Conie,zilimfanya Leythan aogope zaidi.
“Imekuwaje?”
“Sijui,nadhani nimeuwa”
“Unasema?”
“Leythan,tafadhali tukimbie mimi sitoweza kuishi Tanzania.Nataka twende Mombasa”
“Mombasa?”
“Ndio Mombasa”
“Tutafikia kwa nani?”
“wewe twende mimi nitajua”
Kubaki Tanzania kulimaanisha kwenda jela na kufungwa kifungo cha maisha,hakutaka jambo hilo litokee hata mara moja ndiyo maana akapata wazo la kukimbia.

Kitendo cha kupaki gari nyumbani kwake, haraka akashuka na Leythan. Akaenda bafuni na kunawa vizuri, akatoa damu zote mwilini,Leythan akakabidhiwa nguo za kuvaa.
“Kwanza inabidi niende nyumbani,nikapange vitu vyangu”
“Usiku huu?”
“Ndio”
“Naomba nikupeleke”
“Hapana najua unadhani nitakuacha.Conie,siwezi kukukimbia mimi mwenyewe najua nitatafutwa.Nataka kuondoka nawewe pia.Nikukute wapi?”
“Nikitoka hapa naenda ubungo kukata tiketi,najua passport unayo?”
“Ninayo ndio,naomba niende.Nitakutafuta kwenye simu”
“Sawa”
Leythan akatoka mbio.Kazi ya Conie ilikuwa ni kusomba pesa kwenye kabati la marehemu mume wake,akaweka baadhi ya nguo ndani ya begi harakaharaka.Alivyohakikisha kila kitu kipo sawa,akaondoka eneo hilo mara moja,moyoni alijutia lakini hakuwa na jinsi zaidi ya kuiokoa nafsi yake.
***
“Seb…astian nina…ku.fa ni..achiee”
Sauti ya Sonia ndiyo ilikuwa inasikika kwa mbali,akiwa amekabwa shingoni amewekwa ukutani.
Koo lake la hewa lilishindwa kupitisha pumzi,ndiyo maana alikuwa akiongea kwa tabu,kitu kilichomjia mbele yake ni kifo kibaya cha kunyongwa na Sebastian aliyekuwa na hasira mithili ya chui aliyejeruhiwa na mkuki,alijaribu kurusharusha mikono na kumkwaruza Sebastian usoni ili ajiokoe lakini ikashindikana.
Roba alilopigwa lilizidi kumfanya aishiwe nguvu zaidi.Macho yake yakaanza kuona ukungu mbele na taratibu yakaanza kujifumba.Sebastian akazidi kukandamiza mkono wake kwa hasira na ni kweli niya yake ilikuwa kumuondoa Sonia duniani siku hiyo.

***
Picha iliyoonekana ni Sonia kufa tu,hakuwa na msaada mwingine wowote ule aliendelea kukabwa na aliamini huo ndiyo ungekuwa mwisho wake siku hiyo akifia mkononi mwa Sebastian.Brenda aliyekuwa pembeni alishaanza kuogopa,viini vya macho ya Sonia vilianza kupanda juu macho yake yakaanza kuwa meupe,hiyo ikamuogopesha zaidi,moyo wake ukamuuma, hakutaka kuendelea kubaki juu ya kochi kama mtazamaji,akamvaa Sebastian lakini alitulizwa na kifuti cha tumbo kilichomuingia barabara,akajikunja kunja na kukaa kando akiugulia maumivu makali.
**
Ni siku nyingi sana zilipita bila kumtia Sonia machoni,kila siku alikuwa akisema ‘nitaenda kesho, nitaenda Kesho’.Siku hiyo aliamua kufanya kweli,asubuhi kabla ya kwenda ofisini kwake aliamua kunyoosha Sinza.Alivyofika getini aliliona gari la Sonia, lakini nyuma yake kulikuwa na Marcerdez benz pia.
“Kumbe yupo,nimsalime haraka niende kazini”
Dustan akajisemesha na kuvaa koti lake la suti mwilini,akashuka ndani ya gari na kufunga milango.Alivyofungua geti aliona hali isiyo ya kawaida,Mlango mkubwa ulikuwa wazi na alivyoingia kitu cha kwanza ni kumuona Sonia yupo ukutani amekabwa.Kwa harakaharaka alishindwa kuelewa ni kitu gani kinaendelea.
“Soni..a”
Dustan aliita na kumsukuma Sebastian kando,Sonia akadondoka chini kama embe juu ya mti hana nguvu hata kidogo.Dustan ndiye aliyeokoa maisha yake kutoka kifo.Sebastian hakutaka kukubali jambo hilo hata kidogo akataka kumvaa,kama umeme Dustan akachomoa bastola kiunoni na kumuwekea kichwani,lilikuwa ni kosa kubwa sana kufanya hivyo kama mwanasheria lakini hakuwa na namna ilibidi ajitetee.
“You again?”(Wewe tena)
Sebastian alisema,sura ya Dustan haikuwahi kumtoka kichwani mwake alikumbuka kila kitu kuhusu yeye nchini Sweden na ndiye huyu aliyefanya mpaka akafungwa jela miezi sita.
“Back off!”
Dustan akafoka kwa hasira,bastola ikiwa mkononi mwake,kidole kipo kwenye triga.
“Easy,Easy Mr.Hero”
Sebastian alijibu huku akirudi nyuma mikono yake ikiwa juu hewani,sio kwamba hakuogopa bastola, lakini hakutaka kujifanya mnyonge,akajichekesha usoni lakini moyoni alitamani kukimbia mbio.
“Lets go baby”
Hivyo ndivyo Sebastian alivyomwambia Brenda aliyekuwa chini anaugulia maumivu ya tumbo,akamvuta mkono na kutoka naye nje.
“Sonia..Sonia”
Kumbukumbu za Sonia zikawa taratibu zinarudi,akaanza kuona nuru kwa mbali shingo ilikuwa inamuuma kupita kiasi.
***
Ilikuwa ni siku ya Jumatano asubuhi na mapema,Sebastian alikurupuka kitandani jasho jingi likiwa linamtoka mwilini,hakuelewa limesababishwa na nini lakini alijua bado ana hasira mbaya na Sonia.Akahisi kuna kitu kohoni kimemkaba,hasira zilimzidi mwenyewe, akavimba karibia kupasuka, akatembea mpaka kwenye friji na kuchukuwa glasi ili anywe maji,lakini mkono wake ulikuwa unatetemeka kwa hasira.Sura ya Sonia ilipita ndani ya ubongo wake.Kwa hasira alizokuwa nazo akaitupa glasi ukutani ikapasukapasuka.
“Fuc*** you Sonia”
Bado alikuwa na hasira za kumuuwa Sonia,hakuelewa chuki hiyo imetokana na nini.Alivyotupa jicho lake kwenye kioo,ndipo alipochanganyikiwa jina la Sonia kuwa shingoni mwake ndilo likamfanya azidi kukasirika zaidi na zaidi.
Mlio wa Glasi kupasuliwa ulisikika na kupenya kwenye masikio ya Brenda aliyekuwa chumbani kwake,akakurupuka na kutega sikio lake vizuri.Moyo wake ulimuuma, mapenzi aliyokuwa nayo kwa mwanaume huyo yalikuwa hayana kipimo chake.Huwezi kumwambia kitu Brenda likija swala la Sebastian,ndiyo maana hata alivyoambiwa ana ukimwi akachukulia ni kama majungu na fitina tu za kutaka kuwaachanisha na Sebastian wake.
Jinsi alivyo na nguo yake ya kulalia akafungua mlango na kutembea mpaka mlangoni kwa Sebastian na kugonga mlango wake.
“Naniiii?”
Sauti nzito ya Sebastian ndiyo ilisikika kutoka chumbani kwake.
“Kuna nini ndani?”
“Hakuna kitu niache”
“Sebastian fungua basi lakini”
“Unataka nini Brenda?mbona unanigasi gasi”
“Fungua mlango kwanza”
Dakika moja baadaye,kitasa kikacheza Sebastian akatoa sura yake nje,bila Brenda kusema lolote akazama ndani mzima mzima.
“Hee!vipi?”
Glasi iliyovunjika ilimshangaza,ndiyo maana akamgeukia Sebastian na kumuuliza.
“Hakuna kitu”
“Sebastian”
Brenda akaita kwa sauti ya mahaba huku akimsogelea mwanaume huyo,nguo aliyovaa laini inayoonyesha kila kitu ndani isingekuwa rahisi kwa mwanaume yoyote yule rijali kupindua,umbo la Brenda lilivyojikata na chuchu zake zilivyosimama ilimfanya azidi kuvutia mno.Sebastian alibaki tu anamtizama asijue cha kufanya.Hapo ndipo Brenda alipomsogelea karibu na mdomo wake, akatoa ulimi wake akauingiza kinywani mwa Sebastian.Kama kinda la njiwa Sebastian nayeye akaupokea wakaanza kulana denda,mkono wa Sebastian ukapita nyuma ya makalio ya Brenda akaanza kuyabinya,akambeba juu juu na kumbwaga kitandani,akiendelea kumlamba kila sehemu ya mwili wake,shingoni,masikioni na hata machoni.
Damu zao zilianza kwenda mbio na wa kwanza kuzidiwa sana alikuwa ni Brenda,akapitisha mkono wake na kuanza kupapasa gunzi la Sebastian,akalitoa nje na kuanza kulichua taratibu kiasi.Hapo ndipo Sebastian hakuweza kupindua tena akahisi moyo wake unaacha mwili,kazi yake ikawa ni kupapasa maziwa ya Brenda hususani juu ya chuchu,akatoa ulimi wake na kuanza kuyanyonya taratibu.Ni wazi kuwa kila mtu alikuwa hajiwezi kwa mwenzake vitu kama vijidudu vilikuwa vinapita ndani ya damu zao,hawakuwaza kitu kingine bali ni kufanya ngono wakati huo huo.
Sebastian akatoa boxa yake harakaharaka na kumtoa ‘night dress’Brenda, chini alikuwa teyari amelowa na kilichokuwa kinatakiwa kufanyika sio kitu kingine bali ni kitendo cha kuzini.Sebastian akaanza kuseti mtambo wake,ili kuanza tendo.
“Breeeenda,weweee Brendaaaaa.Breeeenda!”
Sauti ya Pendo Jonas ndiyo ilikuwa ikiita tena kwa ukali,iliyojaa kitu cha kusema.Aliita kwa jazba akasikika anagonga chumbani kwa mwanaye,yote hayo Brenda aliyasikia akaamua kuuchuna tu.Akaushika mkungu wa Sebastian ili auingize ndani ya ikulu yake,aliamini kuwa starehe aliyokuwa anataka kuifanya ni bora kuliko kuitwa na Mama yake.
“Breenda”
Mama akazidi kuita,sauti ikawa inasogea mlangoni mwa Sebastian,bahati nzuri kwa Pendo na mbaya kwa Brenda kuwa mlango haukufungwa na funguo,ulivyogongwa mara mbili bila kuitikiwa Pendo akanyonga kitasa.Kitendo alichokishuhudia mbele yake kilimuuma moyo kupita kiasi.Moyo wake ulimuuma sana akahisi unamwagika damu.

***

“Mama shikamoo”
“Marahaba mwanangu, hujambo?”
“Niko sawa Mama, lakini siyo sana”
“Kwanini?”
“Kuna mambo nahitaji kuzungumza nawewe”
“Sasa hivi?”
“Ndio kama ikiwezekana,upo wapi?”
“Nipo Hotelini,nilipofikia”
“Upo na mwanaume mmoja anaitwa Sebastian kwenye hiyo hotel?”
“Ndiyo”
“Naomba nikuone kabla mambo hayajakuwa mabaya Mama angu”
“Sawa,njoo hotelini”
“Hapo siwezi kuja,labda tukutane first inn.Samora Avenue”
“Karibu na Embassy?”
“Ndiyo”
“Sawa Mwanangu”
Sonia alikuwa Simuni baada ya akili yake kumkaa sawa,kila lililotokea aliamini kuwa mdogo wake Brenda ndiyo kafanya hayo yote ingawa hakutaka kukubaliana na jambo ambalo lilikuwa mbioni kutokea,mdogo wake kupata ukimwi kirahisi. Ilibidi afanye kila njia,hakuwa na haja ya kuweka siri ndani ya mtima wake katika jambo hilo la hatari.Vita yake ilikuwa ni yeye na wanaume hasa hasa Sebastian,mchezo wa kulipiza kisasi ulikuwa ni kama unamrudia.Sebastian alikuwa ana mapenzi na Mdogo wake na kwa maana hiyo Ukimwi ulikuwa unarudi katika familia yake mwenyewe,hakutaka jambo hilo litokee.
Aliapia kuwa atapambana mpaka dakika ya mwisho au tamati ya pumzi yake.Ilikuwa ni bora afe kuliko kushuhudia Sebastian anamuambukiza Brenda virusi hatari vya ukimwi alivyompa yeye mwenyewe.
Wakati anawaza hayo Dustan alikuwa tayari ameondoka.Akaingia bafuni kuoga harakaharaka na kuchukuwa funguo za gari,akaendesha kwa kasi mpaka posta, akapaki na kumtafuta Pendo Jonas simuni.
“Mimi mbona nishafika muda,nipo huku juu”
“Sawa Mama nakuja”
Sonia akatembea harakaharaka na kupanda ngazi,alivyopiga jicho lake mwisho alimuona Pendo Jonas, akamsogelea.
“Shikamoo Mama”
“Marahaba mwanangu”
Muhudumu alivyokuja,wakaagiza vinywaji.Hakukuwa na muda wa kupoteza Sonia akamtizama Mama yake usoni,hakujua ni wapi aanzie.Hakutaka swala la ugonjwa wake lijulikane kwa kila mtu,lakini hakuwa na jinsi.Ili kumuweka Brenda salama ilikuwa ni lazima aweke mambo wazi kwa maana hakuwa na sababu nyingine yoyote ile ambayo angeamini angeweza kumshawishi mama yake.
“Mama naomba nikwambie ukweli,pia naomba unitunzie hii siri”
Sonia akaanza kuongea,Pendo akasogeza kichwa chake karibu ili kuambiwa kitu kinachosadikika ni siri.
“Ni kitu gani mwanangu?”
“Mimi ni Muathirika wa ugonjwa wa Ukimwi”
Pendo Jonas akaganda,kitu hicho kilionekana kumshtua, akamtizama mwanaye machoni.
“Sonia”
“Mama naomba uniamini,na ninataka ujue kwanini ninakwambia,nilishawahi kulala na Sebastian”
“Niniiiiiii?”
“Ndiyo hivyo Mama”
Ghafla Sonia akaanza kumwaga machozi,akaanza kuhadithia kila kitu kilichotokea katika maisha yake tangu alivyokuwa nchini Sweden, alivyokutana na Sebastian,na jinsi alivyoteswa nusura kufa.Dakika mbili zilikuwa nyingi kwa Pendo,akaanza kuhisi macho yake yamejaa machozi.Yakaanza kububujika mpaka mashavuni,alisikitika mno na kumuonea huruma sana mwanaye Brenda.Hakutaka kujipa jibu la moja kwa moja kuwa Brenda ana ukimwi pia.
“Sonia Mwanangu”
“Kama unabisha Mama,angalia shingo yake.Ina jina langu,ukweli ndiyo huo tafadhali naomba umwambie.Mimi nilishamwambia lakini sijui kama aliyazingatia ma….”
Sonia alishindwa kumaliza anachotaka kuzungumza,akavuta kiti nyuma na kukimbia kutoka nje, akimuacha Pendo Jonas mwingi wa mawazo,alishindwa kuyaelewa sawasawa maneno ya Sonia.

***
Usiku kucha alikuwa akimsubiri mwanaye bila mafanikio,simu ikawa haipiti akamsubiri mpaka usiku wa manane ili amuonye,kilichomchanganya akili yake pia Sebastian hakuwepo.
Akawa ametulia kitandani tu,japokuwa alipania lakini usingizi ulimpania zaidi,akapitiwa na kuzinduka asubuhi na mapema,glasi iliyopasuliwa ilimshtua kutoka usingizini.
Akasubiri kidogo akahisi mlango wa Brenda unafunguliwa.Na hata alivyokuwa anamuita Sebastian alimsikia pia.Kilichomchelewesha ni kutafuta nguo za kuvaa.
“Pendo.Are you okay?Where are you going?”(Pendo upo sawa,Unaenda wapi)
Sauti ya Santiago ilihoji,Pendo akapata kigugumizi akashindwa kujitetea, akaanza kujiuma uma.Santiago pia alimfanya achelewe,dakika kumi nzima alikuwa akiyajibu maswali ya mzungu huyu mwenye wivu kupindukia.
“Yes.I’m Coming Darling.Give me a second”(Ndio,narudi mpenzi,nipe sekunde)
“A kiss”
Mzee Santiago akategesha mdomo wake,pendo akamsogelea na kumla denda,japokuwa alihisi anacheleweshwa lakini hakuwa na jinsi ilikuwa ni lazima amsikilize mumewe anachosema.
Baada ya kumridhisha,akavuta kanga akatembea haraka kama askari huku akimuita Pendo.Alivyoingia chumbani kwake akamkosa,hapo ndipo akapandisha hasira, akatembea huku akimuita akielekea chumbani kwa Sebastian.
***
“Brenda,unafanya nini?”
Lilikuwa ni swali lililokuwa na jibu la waziwazi,alichokiona alijua kabisa kuwa watu hao walikuwa mbioni kufanya ngono.
“Mamaaaaa”
“Keleleeeeee,njooo”
Bila aibu na wala kumuogopa Sebastian akafoka kwa sauti.
“Mbona unapenda kunitesa Mama?”
“Nakutesa au nakuokoa na maisha yako”
Pendo aliongea kwa kufoka,Sebastian akashindwa kuelewa ni kitu gani kinaendelea.Hakuelewa lugha ya Kiswahili.
“Why are you shouting like that?”(Kwanini unaongea kwa sauti kiasi hiko)
Sebastian,uzalendo ukamshinda akaamua kuhoji.
“I’m not talking to you, son of a bitch!shame upon you.Stay away from my daughter,you know exactly what I’m talking about”(Nyamaza mtoto wa Malaya,huna hata aibu.Kaa mbali na mwanangu,unajua nini nachoongelea)
Ilikuwa ni kama Pendo anamsubiri Sebastian atie neno,ni dhahiri kuwa alikuwa ana hasira naye.Ndiyo maana akampandishia.
“What did you just say?”(Umesema nini)
Sebastian alikuwa ni mwepesi wa kukasirika hata kwa jambo dogo,tayari nayeye alipandwa na hasira.
“Sebastian Please”(Sebastian,tafadhali)
Brenda akajaribu kutuliza gasia,jambo lililokuwa linaenda kutokea halikuwa zuri.Pendo nayeye alikuwa ni mtata.
“Mama,mbona unakuwa hivyo lakini?Niache na Sebastian wangu ninampenda”
Brenda akafoka kwa sauti na kumpandishia mama yake,kitendo kilichotokea kilimkera mno.

***
Leythan aliendelea kutembeza dudu,hata alivyofika nchini Kenya jijini Mombasa,wakina mama walimfurahia na kuambizana kuwa kuna mwanaume wa Kitanzania yupo jijini humo,anaweza mapenzi.Kila mtu alimpapatikia Leythan akitaka tu huduma kingono.Wengine walisafiri kutokea Eldoret mpaka Mombasa,ili mradi kuonja penzi la kijana huyu.Hawakuelewa lolote kuwa wanazidi kuusambaza ugonjwa hatari wa Ukimwi.
Jambo hilo Leythan alilifanya kuwa siri kubwa mno.Conie hakuelewa lolote.Tabia siku zote ni kama ngozi ni vigumu kuibadili,akasahau janga lililomkuta nchini Tanzania la kutaka kutolewa karoti yake.
Kilichokuwa kinamsaidia ni mwili wake uliokuwa wa mazoezi na sura yake nzuri.
“Ndio naitwa Phenny”
“Phenny au Penina?”
“What ever,lakini napendelea sana kuitwa Phenny”
“Una jina zuri,unaishi wapi?”
“Hapo mbele,kwenye ile minazi”
“Nikusindikize?”
“Hapana,usijali kaka”
“Acha bwana,wacha nikusindikize kidogo kwani vibaya,angalia una dimpo nzuri”
“Sawa basi twende”
Tayari alikuwa amemzimia Mwanamke aliyekuwa anatokea Sokoni jioni hiyo,uzuri na makalio ya Phenny vikafanya kiungo chake cha uzazi kisimame.Safari ikaanza ya kutembea adoado walivyofika gizani,habari ikaanza kubadilika.Phenny akashikwa mkono akavutwa nyuma ya mti wa mnazi.Kama umeme Leythan akatoa ncha ya ulimi wake akautumbukiza sikioni mwa mrembo huyu,ambaye alihisi kama amepigwa na shoti ya umeme mwilini mwake.
Nyanya alizoshika na kapu la bilinganya vikapolocha na kudondoka chini bila kujua.Ukimnya wa Phenny Leythan aliuchukulia kama ushindi.Akashusha mkono wake taratibu na kuinua dera la Phenny na kupitisha mkono ndani,akawa anatafuta kitu anachojua mwenyewe.Kazi ya Phenny ilikuwa ni kujinyonganyonga huku akiyafumba macho yake,midomo yao ikakutana wakaanza kulana denda kwa fujo,haraka dera likatolewa kwa juu,hapo ndipo Leythan bila kujali akainama kidogo na kunyanyua mguu mmoja wa Pheny na kuanza kupiga deki bahari,hivyo ndivyo mambo yalivyokwenda.
Kitu kilichofuata hapo kilikuwa hakielezeki kiwepesi,raha zilizidi Phenny akawa ameinama ameshika mti wa mnazi Leythan akiwa nyuma yake,anakizungusha kiuno chake, tango lake lipo ndani ya ikulu.
Kuanzia siku hiyo huo ndio ukawa mchezo wao,wakikutana Sokoni wanamalizana juu kwa juu.
**
Tabia za Phenny zilimchanganya mume wake,kila ifikapo usiku hakutaka tena kushiriki naye tendo,jambo hilo lilimuumiza sana mtima.
“Phenny mimi nina hamu”
“Mume wangu nimechoka”
“Hapana,kila siku nitabaki hivi.Siyo vizuri.Nipe hivyo hivyo”
Mume mtu hakuelewa Somo,alifanya kutumia nguvu akamvua mke wake nguo,bila kumuandaa,akamwingilia kimwili hivyo hivyo, mpaka akamchubua.
Phenny alibaki akilia tu lakini haikusaidia chochote, kwakuwa alimpenda mume wake yote aliona ni sawa.Damu zilimtoka siku hiyo na hakuweza kulala usiku,alikesha kumlaumu mume wake kwa kitendo alichokifanya.
“Sasa ndiyo nini?”
“Niache nilale”
“Umeona umenichubua?”
“Ungetaka mimi nifanye nini?embu ulale uache kuongea”
“Sawa”
Asilimia tisini na mbili za kupata ukimwi zilikuwepo ndani ya familia hiyo na kifo cha Mume wake kingesababishwa na Phenny mwenyewe.
***
“Ah ahs sssh aaaah Ley..tha…n aaaaah mmmh aaaah,kwichi kwichi kwichi”
Kitanda kilikuwa kinanesa,Leythan alikuwa chini,Conie juu yake.Hakutofautishwa na muendesha farasi tena wa mwendokasi!
Picha lilionekana kuwa ndiyo anakaribia kufika kitonga ndiyo maana aliongeza manjonjo na kulalamika.
“Ba…by aaaaaah aaashssss”
Conie ndiyo alikuwa akimalizia mshindo,alivyofika tu.Leythan nayeye akaanza mbilinge, hazikupita hata sekunde moja nayeye akawa tayari,ametulia.Wakaanza kupigana madenda.
“Baby”
Conie ndiye aliyeita kwa sauti ya kudeka.
“Yes Honey”
“Mbona kila siku unakuwa mpya?”
“Mpya kivipi?”
“Yaani unakuwa mchalo”
“Haa!Haaa!Haaaa! mchalo ndiyo nini?”
“Hujawahi kulisikia lile tangazo,mchalo kawa mtaaamu”
“Kwahiyo mimi ndiyo mtamu?”
“Kuliko asali”
Conie alimwaga sifa,akiwa amekumbatiana na mpenzi wake,kwa mahaba aliyopewa alisahau kabisa kama alimuua mume wake nchini Tanzania,hakutaka kujua chochote kilichoendelea ndiyo maana hata akabadili namba za simu mpaka jina lake.
“Baby,inabidi ubadili jina nawewe,tufunge na ndoa ili wasitushtukie”
“Mh!kwahiyo ndiyo tumeamua kuishi huku mazima?”
“Ndiyo maana yake,wakishtuka tunahama,Tunakuwa kama ndege.Nataka nifungue saluni ili pesa izunguke”
“Mimi nakusikiliza wewe, Master plan”
Wote wakacheka na kupigana mabusu,baada ya hapo walielekea bafuni kuoga.Kifupi Conie na Leythan walikuwa ni kama mtu na mume wake, japokuwa ndoa haikuhalalishwa.

*****

Katika maisha yake alikuwa anafanya vitu viwili tu,kugawa ukimwi na kuhakikisha anakuumiza moyo kimapenzi.Akajifanya kumpenda sana Raphel mwanaume wa chuo cha IFM,kwa Raphael kwake aliona kama ameokota embe chini ya mti wa mpera,Sonia alikuwa mzuri mno.Pesa za matumizi yaani ‘pocket money’ zote alimuhonga Sonia.
Akajihesabia huyo ndiye mke wake mtarajiwa,kilichomchanganya zaidi Sonia alivyomuhaidi kwamba atabadili dini kwa ajili yake.
“Kweli Happy?Utabadili dini?”
“Huniamini?”
“Ninakuamini mpenzi,ile elfu ishirini niliyokutumia ilikutosha?”
“Usijali,ilinitosha”
“Nakupenda sana”
“Hata mimi,nakupenda Raphael.Utanioa kweli au umenitamani tu?”
“Niamini Happy,kama upo tayari nitakupeleka kwa wazazi wangu Tanga,huu mwezi wa Ramadhan ukiisha tu”
“Insha Allah”
“Ha! Haa! Haaa! Haaaaa!ushaanza kujifunza kiislam tena”
“Nakupenda Raphael ndiyo maana”
Ni bora angezingatia masomo na kuweka elimu mbele,tayari maisha ya Raphael yalikuwa hatarini.Katika moyo wake alijiwekea tayari ana mke.Ili kumzuzua kabisa, Sonia alianza kuvaa ushungi na wakati mwingine baibui wakikutana,hiyo ndiyo ikampagawisha zaidi Raphael akaona ni kweli anapendwa!
***
“Sasa wewe Raphael,huyo demu umesema umekutana naye Facebook,alafu unadai anakupenda.Una akili wewe?”
“Siyo Facebook ni Instagram”
“Yote sawa,Mse** nini.sasa ndiyo unaongea nini,yaani demu unakutana naye mtandaoni unasema anakupenda”
“Musa eeh,nikaushie basi mwanangu,umekuja kufturu au kunisimanga?”
“Mimi nakwambia ukweli,nipe maji ya kunawa mikono,tende ziko wapi nianze nazo”
“Subiri zinakuja”
Sonia aliyekuwa jikoni anatengeneza uji aliyasikia maongezi yote,akatabasamu na kuendelea kupika na kukoroga uji.Alimsikitikia sana Raphael aliyekuwa bado mdogo kufa lakini hakuwa na jinsi ya kubadili jambo aliloanza,aliwachukia wanaume.
“Nani analeta?”
“Happy”
“Kwani yupo?”
“Tatizo unaropoka ropoka ovyo”
“Duu,kanisikia nini?”
“Kula bwana”
Dakika mbili zilikuwa nyingi Sonia akaleta tende pamoja na uji.Mussa alivyogeuza shingo alibaki ameduwaa na kijiko cha futari mdomoni,Uzuri wa Sonia ulimzuzua.
“Musa,vipi?”
“Hapana,sio kitu”
Kila kitu kiliandaliwa mezani,ndani ya chumba cha Raphael.
“Baby,mimi naenda”
“Vipi wewe huli?”
“Hapana nimechelewa,nyumbani sijaaga.Nakupenda Raphael”
Akasogeza mdomo wake wakaanza kulana denda,alifanya hivyo makusudi ili Mussa aone.Ilikuwa nayeye lazima awekwe kwenye mtego wake.

****

Nyumba ya Sinza aliiuza kimnya kimnya,akanunua nyingine Mikocheni B, kwa pesa alizokuwa nazo haikuwa kitu kikubwa kwake,aliamini kuwa angeendelea kubaki Sinza,angesumbuliwa na Sebastian Aidan Waytte,vita yao bado ilikuwa kubwa mno,watu hawa walikuwa kama Paka na panya.
Ghafla sura ya mdogo wake Brenda ikamjia,akachukua simu harakaharaka na kumtafuta hewani.
“Brenda,hujambo mdogo wangu”
“Sijambo,vipi?”
“Kwani tuna ugomvi?”
“Sijui”
“Sikiliza nikwambie mdogo wangu,zingatia niliyokwambia”
“Dada Sonia,naomba uniache na maisha yangu tafadhali.Mbona mnakuwa hivyo”
“Brenda,nakupenda mdogo wangu”
“Sitaki,niacheni nife”
“Lakin…tititi”
Alishaongea na kuchoka kabisa,akaamua kuyaaacha mambo kama yalivyo.
“Eh Mungu mdogo wangu,sitaki afe kwa kifo hiki kibaya.Sijui nifanye nini?”
Sonia aliwaza na kushindwa kupata jibu la harakaharaka,kichwa chake kilivurugika kwa kiasi cha kutosha.

****
“Nitahakikisha kwamba Tanzania tunachukuwa kombe la Dunia,mpaka tulipofika ni jambo la kumshukuru Mungu”
“Ni changamoto gani mlikuwa mnapata huko Ujerumani?”
“Zipo nyingi,kwanza wale watu ni wabaguzi.Wana dharau sana.Sio mbaya tukawaonesha kuwa Tanzania ya mwaka arobaini,sio ya sasa hivi”
“Kitu gani ambacho unataka kuwaambia Watanzania,wanaokuangalia sasa hivi Partson Ngogo”
“Support yenu,tuwe wazalendo.Wenzetu ni wazalendo sana.Tanzania tuamke jamani”
“Sasa hivi mnatarajia kucheza na timu gani?”
“Mwezi ujao tunacheza na Senegal”
“Sasa unatuhaidi nini?”
“Mimi siwezi kuongea maneno mengi,Watanzania wasubiri tu”
Waandishi wengi walimsonga Partson Ngogo na kumgasi.Kikosi cha Tanzania kilikuwa kimerudi nyumbani, kutokea nchini Germany,habari nzuri ni kuwa waliwafunga nje ndani.Na magoli mengi yalisababishwa na Partson Ngogo,makocha mbali mbali nje ya nchi walianza kumgombania na kupanda dau wakitaka kumsajili katika timu zao.
“Jamani tunaomba njia tafadhali”
Askari wakawatoa watu,kila mtu alitaka kumshika mkono Partson Ngogo,kifupi umaarufu wake ulimzidi umri.
***
Sonia alisikia kichefuchefu cha kutapika baada ya kumuona Partson kwenye luninga,akajisikia hasira kupita kiasi,akashindwa kuzima televisheni.Alibaki akimwangalia tu.Hakujua ni kitu gani akifanye,fikra zake zikarudi nyuma kwa kasi,akamuona alivyomfumania.
Partson ndiye aliyesababisha mpaka atake kujiua nchini Afrika Kusini.
“Nimrudie nayeye nimpe Ukimwi?”
Sonia akawaza.
“Hapana,Tanzania inamtegemea sana.Hata hivyo sijali nitajua cha kufanya,dawa yake ipo jikoni”
Sonia aliwaza na kuzima televisheni,akaingia bafuni na kujimwagia maji,akavaa nguo za kulalia na kujitupa kitandani,kila alivyojigeuza usingizi haukuja.
“Leo Ijumaa kumbe,woow naenda Maisha club,leo sitaki shobo na mwanaume yoyote ile”
***
Spika zilikuwa zinakita kupita kiasi,wanaume kwa wanawake walikuwa katikati wamejichanganya wanabambiana wanaruka majoka, ndani ya ukumbi wa Maisha,mambo yalikuwa raha mustarehe.
Wasichana wengi walivalia nguo fupi,vitovu nje.Ulikuwa ni usiku mnene.
“Nasraaaaa,ndio unaondoka au?”
“Ndiooo”
“Baki baki basi kidogo bwanaaa”
“Hapana,nawahi homeee,kesho asubuhi naenda kufanya interview”
Mr.Alex Mwandambo ndiye alikuwa kaunta,yaani viti virefu anakunywa mvinyo huku akitingisha kichwa chake,akienda sawa na mziki unavyodunda.
“Njoo basi nikupe pesa ya Taxi”
“Sawa”
Akasimama kidogo na kutoa pochi,akatoa shilingi laki tatu.
“Hii ni nauli ya kesho pia,tukutane kwa siku zote”
“Poa baby”
Nasra,akageuza shingo yake na kutoka nje,mlangoni akagongana kikumbo na Mwanamke aliyevaa kikaptura kifupi kashika funguo za gari.
“Dada samahani,sijui nakufananisha”
Sonia akamuuliza Nasra.
“Hapana”
“Kweli?”
“Sidhani,anyway nina haraka”
Nasra akaondoka.
Lakini Sonia katika kumbukumbu zake sura hiyo haikuwa ngeni ingawa alishindwa kumkumbuka vizuri.
Kitendo cha kuingia ndani macho ya wanaume yote yalikuwa kwake,kila mtu alimkodolea macho.Kitu hicho kilikuwa cha kawaida kwake,akatembea mpaka kaunta na kuvuta kiti kirefu.
“Nipe Redwine tafadhali”
“Sawa”
“Sio kwenye glasi,nipe mzinga mzima”
“Okay”
Sonia aliwekewa chupa kubwa,akafungua na kuimimina ndani ya glasi.
“Hafuan,ni weewe?”
Mr.Alex Mwandambo aliita huku akimshangaa Sonia.


***

Alikuwa yupo radhi kufanya chochote ama kugombana na Mama yake kwa ajili ya Sebastian,hakuwa tayari kuachana naye kwa njia moja au nyingine.Mama yake alishaongea mpaka kuchoka lakini ilikuwa ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa acheze mziki.
Brenda hakumsikiliza mama yake,aliweka masikio yake pamba.Hakuna siku ambayo Pendo hakuweza kuisahau katika maisha yake,alivyotukanwa na Sebastian baada ya kuwafumania.
“Get out, bitch”(Toka nje Malaya)
Sebastian alitamka bila kujali anaongea na mtu wa aina gani mbele yake japokuwa Brenda alisikia lakini hakujali,aliendelea kumuunga mkono Sebastian.
“Mama naomba uwende,tuache”
Brenda nayeye akatia neno.Pendo alilia machozi hakuamini kitu alichoambiwa na Mwanaye.
Aliondoka kimnya kimnya akijisikia aibu,hata alivyorudi chumbani kwa mume wake alikosa raha ya maisha.Mr.Santiago alimuuliza lakini hakutaka kumuweka wazi kwa kitu kilichotokea dakika mbili zilizopita,hakutaka kuamini kuwa Mwanaye anaenda kufa na ugonjwa wa Ukimwi,alikuwa ana mtoto mmoja peke yake.Hilo ndilo lilimuuma Zaidi.
***
Shangwe zilikuwa nyingi ndani ya club,mziki ulizidi kuwa mkubwa mno.Wasichana kwa wavulana wazee kwa vijana walikuwa katikati wanazungusha viuno,wengine wakiwa wamekumbatiana.
Sonia hakuwa na hamu ya kucheza siku hiyo, ndiyo maana alibaki kaunta akiwaangalia watu wanavyocheza,hapo ndipo alipokutana na Mr.Alex Mwandambo.
“Hafuan”
Kwa mara ya kwanza hakudhani kama ndiye yeye anaitwa.Mpaka alivyoshikwa bega na kugeuka.
“Hafuan,ina maana hunisikii?”
“Sikukusikia”
“Vipi,ushanikumbuka?”
“Sura yako,sio ngeni”
“Alex,nilishawahi kukupa lifti nikaku..”
“Alright,nishakukumbuka,za siku nyingi?”
“Nzuri,ni kama bahati leo kukutana na wewe mahali hapa”
“Kwanini iwe bahati sasa?”
“Ngoja basi wakuongeze kinywaji”
“Hapana,mzinga huu siwezi kuumaliza”
Macho ya MR.Alex yalitua juu ya mapaja ya Sonia yaliyokuwa manene meupe,kaptula fupi aliyovaa ilimfanya azidi kuwa kivutio,moyo wa Alex ukaingia majaribuni.
Alivyopiga jicho lake kifuani mwa msichana huyu ndiyo kabisa,nusu ya kifua cha Sonia kilikuwa wazi,hiyo ndiyo ikawa tatizo lingine.Alex akawa ana maneno ya kuongea lakini hakujua ni wapi aanzie.
“Hafuan”
“Abee”
“Unaishi wapii?”
“Hapa hapa Dar es salaam,nisubiri nakuja”
Sonia akasimama,hapo ndipo Alex alibahatika kumuona vizuri,kiuno cha Sonia kilibinuka na mbali na hapo aliona cheni iliyovaliwa na Sonia kiunoni,hiyo ikampagawisha zaidi.
“Mh,nitatoka kweli hapa leo?Msichana huyu ni mzuri khaaa,jamaniii”
Alex akajisemesha mwenyewe huku akimtizama Sonia akipotelea gizani.Kilichomtuma akilini mwake ni ngono tu,tamaa zilimuingia damu yake ikamuenda mbio.
“Hey,nipatie Konyagi kubwa”
Alex alimwambia muhudumu wa baa.
“Kisichana au?”
“Mzinga mkubwa”
Mzinga ukaletwa Alex akaufungua,hazikupita hata dakika mbili Sonia akatokeza.
“Nakuongeza Konyagi”
“Noo,Please”
“Kidogo bwana”
Alex alianza kuongea huku akimimina kinywaji hicho kikali ndani ya glasi ya Sonia,niya yake ilikuwa ni kumlewesha azime amfanye vitu anavyojua yeye,aliamini kuwa wanawake mbele ya pombe hawajiwezi na hawana kauli.
Pombe ziliendelea kunyweka,ni kweli Sonia alianza kuhisi kizunguzungu kikali.
“Aleeeeex,mimi naaaondokaaaa”
“Wapi?acha nikupeleke”
“Unipelekee wapiiiii?”
“Kwako”
“Hupajuuiiii bwanaaaa,Godbye”
Sonia akasimama na kuanza kuyumba,Mr.Alex akaanza kumfuata kwa nyuma huku akijifanya kumpa msaada,walivyotoka nje Sonia akasimama.
“Wewe Mse*** embu niaaacheee,unataka kunifanyaaaa nini?”
Sonia aliongea kwa ukali,siku zote akilewa anakuwa mkali kuliko chachandu.
“Nakupeleka kwako Hafuan,hali yako sio nzuri”
“Embuuuu,Don’t touch meeeee,hee! heee! heeeeee! heeeeee! Usijaribu kunishikaaaa,nani kakwambia nimelewa?Do i look like someone who needs help?Hell no,pleaseee goo,najua ninapoenda.Niache usiniletee Use*** unataka kunipeleka wapi?Usinishike kiunooo stoop”
Ilikuwa ni bora umtongoze Sonia akiwa mkavu,ajaonja aina yoyote ya kilevi kuliko akiwa bwii,alikuwa ni mkorofi na mwenye matusi,hiyo yote alikuwa anajihami.Ni wazi kuwa alielewa amelewa sana,hakuwa na uhakika kama atafika salama nyumbani kwake, Mikocheni.
“Hafuan,unaenda wapi huko sasa?”
“Parking,Gari yangu iko wapiiiiiii,gari yanguu iko wapi?Wewe falaaa askari”
Sonia alikuwa akielekea barabarani na sio kwenye maegesho ya magari.
“Huko sio Parking”
“I said Nooooo,usinishike.Snelaa snelaaa.Fuc** you”
Aliongea mpaka kiswiden,kweli pombe sio chai.
Kila aliyemuona alimtupia matusi walinzi pia walioga maneno machafu ya Sonia,akatoa funguo zake za gari mfukoni na kubonyeza rimoti baada ya kufika parking na kuliona.
“Oh,Alex See you Tommorow my friend,it was nice to see you todaaaay,Byeeeeee”
Sonia aliaga na kufunga mlango wa gari kwa nguvu,akaweka funguo na kuliwasha.
Jinsi alivyolitoa alimanusura mlinzi agongwe.
“Kahaba wewe,ungenigonga je?”
Mlinzi akatoa matusi baada ya kujitupa kwenye majani,alivyokoswa koswa na gari.
“Kahaba baba yako mzaziiiii”
Sonia nayeye akajibu akiwa ndani ya gari.Mshale wa spidi ulizunguka na gari ikazidi kwenda kasi,kwa kuwa usiku ulikuwa mwingi, barabarani hakukuwa na msongamano wowote ule wa magari,ndiyo maana alipeta.Japokuwa alilewa sana lakini njia ya nyumbani aliitambua tena akafika salama salmin!
****
Ugonjwa wa Pedeshee Kway ulikuwa wa kusikitisha mno,aliteseka kwa takribani miaka mitano kitandani,alikondeana kupita kiasi.Pesa alikuwa nayo ya kutosha lakini hazikumsaidia chochote,kutokana na hali yake kuwa mbaya zaidi hakuruhusiwa kusafiri kwenda popote pale.
Alikuwa akisubiri kifo chake kitandani.
Ugonjwa wa virusi vya ukimwi uliuwa kinga zote za damu yake,alikohoa na kutema mabundu ya damu.Usingeweza kuamini kuwa huyu ndiye Mwanaume aliyekuwa anatesa na kutingisha kwa pesa Afrika mashariki na kati.
Mke wake Kim kila siku alilia, alijua maana yake,sababu aliamini kuwa baada ya mume wake kufariki yeye ndiye angefuatia.Dalili hizo zilionekana wazi sababu hata yeye alianza kukohoa mara kwa mara,alilia machozi, kuwaacha watoto wake wadogo.
“Honey I’m so sorry,it was my fault”(Mpenzi nisamehe,yote ni kwasababu yangu)
Pedeshee Kway alimuambia mke wake siku hiyo Usiku akiwa anapewa uji.Mwanamke huyu wa Kizungu alimpenda Pedehee Kway na alikuwa naye bega kwa bega.
“It is okay Darling,you don’t have to regret.You have me”(Usijali mpenzi,hutakiwi kujuta,upo na mimi)
“When i die today,tell My daug..hter Michelle how much I lo..ve h..er.I want to see my Son Aron today”(Kama nikifa leo,mwambie binti yangu Michelle kiasi gani ninavyompenda.Nahitaji kumuona Mwanangu Aron leo)
“Today?”(Leo)
“Yes swea..heart.Make it hap..pen. koho..kohoo”(Ndio mpenzi,fanya iwezekane)
Pedeshee Kway aliongea na kukohoa,alikuwa amekondeana mno,kichwa tu ndicho kilichobaki.Alisikitika sana kuacha utajiri aliokuwa nao duniani.
Aliumia zaidi kwasababu hakukuwa na mtu yoyote yule kati ya marafiki zake aliyefika kumuona,mzigo huo ulikuwa wake na mke wake tu.

Kwa jinsi alivyodhoofika mwili hakuweza hata kujigeuza upande wa pili,mke wake ndiye aliyefanya hayo yote,alimuogesha na kumfanyia kila kitu hapohapo juu ya kitanda,akisaidiwa na baadhi ya madaktari walioajiriwa kumuuguza Pedeshee Kway.
**
“Aron,Baba yako anakuita”
“Baba?”
“Ndiyo”
“Mamaa,nimeshakwambia sitaki kumsikia Baba katika maisha yangu.Sitaki kusikia”
“Aron nisikilize, hata kama mimi niligombana naye.Ugomvi wangu ni mimi nayeye.Tafadhali nenda.Tiketi itatumwa”
“Lakini Mama,uliniambia Baba alikutelekeza,sasa inakuwaje tena?”
“Ndiyo alinitelekeza mimi,hupaswi kumuwekea chuki.Jifunze kusamehe mwanangu”
Maneno hayo yalitoka kwa Mwanamke mwenye macho makubwa kiasi mnene wa umbo.
“Mama”
“Aron,nenda tu”
“Hapana labda twende wote,siwezi kwenda mwenyewe”
***
Ilikuwa ni mwaka 1989,shule ya Sekondari Jangwani. Shule hiyo ilipakana na shule ya wavulana Azania,ilitenganishwa na ukuta mkubwa.
“Kway”
“Naam Julia”
“Nikwambie kitu”
“Kitu gani?”
“Nina mimba yako”
“Unasema?”
“Hujanisikia?Nina mimba yako”
Wote walikuwa wanafunzi tena wa Sekondari, ni jambo ambalo lilimchanganya sana Kway,habari hizo kwake zilikuwa za kutisha.Picha iliyomjia kichwani mwake ni wazazi wake walivyokuwa wakali mno,hakuelewa angewaambia nini wamuelewe.
“Sipo tayari wewe unajua home kulivyo,dingi mkali”
“Sasa nitafanya nini?”
“Wewe itoe tu”
Swala hilo lilikuwa gumu sana kwa Julia,alishasikia nini madhara ya kutoa mimba,aliogopa kufa akiwa bado mdogo.Hapo ndipo mapenzi ya watu hawa wawili yalipokomea.
Kway hakutaka kumsikia tena Julia katika maisha yake.Haikupita miezi miwili Kway akasafiri kwenda India kusoma huku nyuma akimuacha Julia anateseka na Mimba,miaka mingi ilipita bila kufanya mawasiliano yoyote yale.
Baada ya miaka kusogea alivyomaliza,akaajiriwa na kupata pesa ambazo zilimpa kiburi,hata alivyosikia ana mtoto Tanzania anaitwa Aron, alimpuuzia.
***
Alihisi angefanya makosa bila kumuona mtoto wake Aron ambaye hakuwahi kumuona kwa macho,ndiyo maana alitaka kumuaga kabla ya kifo chake cha kuteseka.Usiku wa siku hiyo ndiyo Pedeshee Kway alizidiwa kupita kiasi,kifua kilimbana akashindwa kuhema japokuwa aliwekewa mtungi wa gesi,mke wake Kim aliangua kilio.
Hakuna hata mmoja aliyeweka matumaini kuwa atafikisha siku inayoitwa kesho.
“Ki..m usha..tuma Ti..keti?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Pedeshee Kway.
“Ndio Mume wangu,lakini wataingia kesho”
“Nat..ese..ka sa..ana.Natamani kufa”
“Usiseme hivyo”
“Na..kufa”
Kweli kifo cha ukimwi kinatesa mno,maumivu aliyokuwa anahisi Pedeshee Kway yalizidi kipimo.
Alitamani asimame juu ya mbingu auambie ulimwengu mzima jinsi kifo hicho kinavyoumiza.
***
Julia na Mwanaye Aron waliingia nchini Kongo Kinshasa,asubuhi sana siku inayofuata.Hawakukawia, ujio wao ulijulikana,wakapokelewa na dereva aliyetumwa.
Waliingia ndani ya ngome ya Pedeshee Kway baada ya dakika arobaini,jumba lake kubwa lilifananishwa na kasri anayoishi mfalme.Siyo Julia wala Aron wote walilishangaa jumba hilo kubwa.
Mlango wa gari ukafunguliwa wakashuka.
“Mom, they have arrived”(Mama,wameshafika)
Mmoja wa walinzi alimuongelesha Kim.
“Okay”
Chumba cha Pedeshee Kway kikawekwa vizuri.Julia na Aron wakaingia,huruma iliwajaa.Peeshee Kway alibaki mifupa tu,hakuwa na nywele kichwani.
“Ar..on kohokohoooo”
Julia alivyomuona tu alimwaga machozi,japokuwa hakuwa na uhakika na ugonjwa anaoumwa Pedeshee Kway lakini alihisi,dalili za ugonjwa wa Ukimwi zote alikuwa nazo Kway,hilo lilikuwa wazi.
“Juli..a nisameh..e nimefur..ahi kukuo…na mi.mi mim.. ndiy…”
Sentensi haikuisha,akaanza kukakamaa na kutulia.Huo ndiyo ukawa mwisho wa Pedeshee Kway, duniani.
***
“Stop her!”
Sebastian ndiye alikuwa akipiga kelele,akimkimbiza Sonia barabarani,wengi walidhani watu hao wanacheza tu.Ndiyo maana hawakutaka kuwa na muda nao,walibaki wakiwashangaa,kukamatwa kwa Sonia kulimaanisha apigwe vibaya sana.
Hakuelewa nguvu za kukimbia alizitoa wapi,zilikuwa ni mita chache tu zilibaki ili akamatwe.Sebastian alimkimbiza kwa hasira na usongo huku akiwapiga watu vikumbo.
“Mwiziiiii,nisaidieni”
Msaada aliokuwa anaomba Sonia,haukusaidia kila mtu alimtizama.Mbele yake alimuona Mwanaume mrefu kiasi,anafungua gari bila kuuliza nayeye akafungua mlango wa kushoto na kujifungia ndani.
“Vipi?”
“Kaka nisaidie tafadhali,kuna mwizi”
“Unasema?”
“Funga mlango”
Mlango wa gari ukafungwa,Sebastian akafika nje ya gari akabaki akigonga kioo.
“Mbona sikuelewi binti?umeiba nini?”
“Nitakueleza,naomba niokoe.Kaka mimi sijaiba”
“Unaelekea wapi?”
“Sijui twende tu”
Gari likaanza kuondoka,Sonia hakuamini kama amepona kwa mara nyingine.Alikuwa akihema juu juu huku akiwa anaangalia nyuma akimuangalia Sebastian akiwa amesimama kashika kiuno.
“Kaka ahsante sana”
“Usijali,imekuaje?”
“Ni stori ndefu,kifupi naitwa Phelista”
“Mimi naitwa Aron,Aron Kway”
Moyo wa Sonia ukapiga kwa nguvu,akageuka na kumuangalia vizuri mwanaume huyo.Jina hilo halikuwa geni kwake,kumbukumbu zake zikaanza kujikusanya ni wapi alilisikia.

***
Ndani ya gari ukimnya ulizidi kutawala,bado Sonia aliendelea kuzivuta kumbukumbu zake nyuma akikusanya vitu mbalimbali lakini jina hilo liligoma kuja ingawa alishawahi kulisikia kabla.Wakati akiwa anawaza hayo kulikuwa kuna ukimnya ndani ya gari.
“Kaka ahsante sana,naomba usimame hapa”
Sonia akavunja ukimnya.
“Nisimame hapa?”
“Ndio”
“Okay”
Gari likawekwa kandokando,Sonia akashukuru mno akabaki amesimama na kulishuhudia gari la Aron linaondoka,akatembea mpaka stendi ya mabasi.Bado alishindwa kuelewa ni wapi alipo.
“Kaka samahani”
“Bila samahani”
“Hapa ni wapi?”
“Kwa warioba,Mikocheni”
“Okay ahsante”
Mfukoni hakuwa na pesa yoyote ile,lakini alitakiwa afike nyumbani kwake.Alivyoona bajaji nyuma yake akatembea mpaka zilipo.
“Mikocheni B”
“Sehemu gani?”
“Twende nitakuelekeza karibu na kwa Rwakatale”
“Poa ingia”
Sonia akaingai ndani ya Bajaji akiwa na wasiwasi mwingi,alimuhofia sana Sebastian katika maisha yake.Hakuelewa ilikuwaje akakutana naye barabarani.
Baada ya dakika kumi na tano bajaji ikasimama nje ya geti kubwa la rangi ya kijani.
“Kaka nisubiri nakuletea pesa yako”
“Sawa,usiniweke basi sista”
Haikuchukuwa hata dakika Mbili Sonia akarudi na pesa ya dereva wa bajaji.
***
Siku hiyo hakutaka kutoka nje,alishinda tu ndani na kanga moja peke yake.Kazi yake ilikuwa ni kuingia mitandaoni kuangalia meseji zilizoingia na kuchunguza watu mbalimbali.Akaangalia picha alizopiga na kuziweka mitandaoni na kutabasamu,zilisifiwa sio kawaida.
“Leo nataka kuwaambukiza wanaume kama wawili hivi Ukimwi”
Sonia akajisemea,akapandisha kanga yake juu vizuri mapaja yake yakawa wazi akatembea mpaka kwenye kioo na kujipiga picha.Hakuchelewa akai ‘post’ facebook.
Ndani ya dakika thelathini ilikuwa na ‘comments’ mia mbili,akimwagiwa sifa kemkem.
“WENGINE TUMEFUNGA BWANA”
Hiyo ndiyo moja ya ‘Comment’ iliyomfanya Sonia afurahi.
“Ndiyo naanza na huyuhuyu,leo utafungulia tu”
Sonia akajisemea na kuanza kumpekua kijana huyo,akaingia kwenye picha zake.Uzuri alikuwa akiishi jiji la Dar es salaam.Akaingia inbox na kumtumia Meseji.
“NASEER,MAMBOZ”
Sonia akaanza kwa kutuma meseji,huku akisubiri jibu.Pepo lake la kuambukiza Ukimwi lilikuwa linamuwasha.
“POA,VIPI?”
“SAFI,SAMAHANI KWA KUKUHARIBIA SWAUMU”
“USIJALI VITU VINGINE UWE UNAAGALIA”
“NISAMEHE BURE,SIKUJUA.TUNAWEZA KUWA MARAFIKI?”
“NGOJA NIKASWALI”
“SUBIRI KWANZA NIKUTUMIE PICHA ZANGU NYINGINE NZURI”
Sekunde hiyohiyo Sonia akatuma picha tatu,aliamini kwa picha alizotuma hata angekuwa mwanaume mtata kiasi gani,angetingishika.
“MH”
“VIPI,NASIR?”
“HUYO WEWE?”
“NDIYO”
“SIO KWELI,NYIE MADEMU WA FACEBOOK MARA NYINGI PICHA ZINAKUWA SIO ZENU”
“SINA SABABU YA KUWEKA PICHA YA MTU”
“UNAISHI WAPI?”
“KEKO MACHUNGWA”
“ACHA UTANI BASI”
“KWELI TENA”
“MIMI MBONA NIPO KEKO,MAGOROFANI HAPA”
“UNANIDANGANYA”
“KAMA UNABISHA NJOO”
Nasri alikuwa katika majaribu makubwa mno,tena katika mfungo wa ramadhan.Picha za Sonia zilimpagawisha kupita kiasi,hakuelewa kuwa alikuwa mbioni kwenda kuuliwa taratibu na ugonjwa harati wa Ukimwi.
Angelijua wala asingeendelea kutumiana Meseji na Sonia.
“MIMI NAOGOPA”
“USIOGOPE,NJOO MUDA WA SAA MBILI USIKU”
“POA”
Kazi ya Sonia ikawa imeishia hapo,akaweka tiki kuwa tayari kashapata kitoweo.
“Wanaume wataacha lini upumbavu,kwa staili hii si nitawauwa wote”
Aliwaza na kujitupa juu ya kochi,alisikitika sana na kuwaonea huruma wanaume lakini hakuwa na uwezo wa kuyabadili mawazo yake.Mama yake alikufa kwa kuteseka na ukimwi kitandani ni wanaume ndiyo walimuambukiza,alizidi kupata hasira zaidi na zaidi.
***
“Ah ah ah ah ah shs aah aah sshss”
Brenda ndiye alikuwa akitoa sauti za puani,miguu yake yote miwili ilikuwa imetanuliwa huku na kule wakiwa uchi wa mnyama na Sebastian.Ikulu yake ilikuwa inapigwa deki ndiyo maana alitoa kila aina ya miguno, kazi yake ilikuwa ni kujigeuza huku na kule,akishika mashuka na kuyatandua.
Kwa jinsi alivyokuwa akifanyiwa aliamini kuwa yupo sahihi kumtukana mtu yoyote atakayeingilia mapenzi yake na Sebastian,raha alizokuwa anapewa hakuweza kuzifananisha na kitu chochote kile chini ya yua jua la Mungu,alihisi yupo angani anaelea, vitu vyote anaviona kwa chini.Alihema juu juu kwa raha huku akikikandamiza kichwa cha Sebastian ndani kabisa ya mgodi wake,mambo aliyofanyiwa yalikidhiri.
Alilambwa kila sehemu ya mwili wake kuanzia shingoni,masikioni mpaka pua.Kwa Brenda mpaka inafikia hatua hiyo akashindwa kuvumilia alikuwa hajiwezi tena,akaupitisha mkono wake taratibu akashika karoti ya Sebastian,akamvuta karibu na kuiingiza ndani ya mgodi wake taratibu,kila ulipozidi kuingia ndipo alipozidi kuhisi raha zinazidi zisizokuwa na kipimo chake.
***
Pendo hakuwa na raha ya maisha,kila alipomfikiria mwanaye Brenda aliumia moyo.Hakutaka kuamini kuwa mwisho wa siku atakuja kufariki kwa Ugonjwa hatari wa Ukimwi,alivyomkumbuka Marehemu Nickson miaka ya nyuma,aliumia moyo.Kila siku alijifungia chumbani akilia tu.
Mume wake Mr.Santiago aliingiwa na mashaka ilimbidi amsaili.
“Vipi mke wangu,mbona hauna raha?”
“Niko sawa Santiago”
“Sio kawaida yako”
“Usijali Mpenzi wangu”
“Tunakaribia kuondoka,niliongea na Waytte juzi anasema tuna kama wiki mbili zimebaki turudi Marekani”
“Vizuri”
Pendo aliitikia kwa kifupi,huku akilengwa na machozi.Hiyo ndiyo ikamfanya Mr.Santiago atake kujua zaidi.
“Haupo sawa Pendo,una tatizo gani?”
“Ni mambo makubwa Mme wangu”
“Yapi hayo?”
Kila Pendo alipotaka kutoa kitu kilichokuwa ndani ya kifua chake,moyo wake ukawa una sita.Hakuelewa ni kwanini,alitamani apewe ushauri na mtu yoyote wa karibu.
“Nitakwambia siku nyingine”
“Hapana Pendo,niambie sasa hivi”
Pendo Jonas alimuangalia mume wake kwa kama Sekunde tano machoni,moyo wake bado ulikuwa mzito mno kutoa kitu kilichokuwa ndani ya kifua chake.Mbali na hapo swala la Sonia kuwa na virusi vya ukimwi lilitakiwa liwe siri ndiyo maana akawa anasuasua!
“Mpenzi”
“Abee”
“Niambie nambie kianachokusumbua,nitakusaidia hata kwa mawazo”
Bado alibishana na nafsi mbili moyoni mwake,ya kwanza iligoma ya pili ikawa inamwambia aseme ili apewe ushauri.Kati ya vitu viwili ilibidi achague kimoja,nafsi ya pili ilionekana kuwa na nguvu na ushawishi mkubwa mno.
“Ni kuhusu Sonia”
“Sonia?Ndiyo nani?”
Hapo ndipo alipokumbuka kuwa,Mr.Santiago hajui lolote.
Jinsi mambo yalivyokuwa yameenda na hali ilipofikia ilibidi amuhadithie Mume wake kila kitu kinagaubaga!hakumficha chochote akamuanzia jinsi mambo yalivyokuwa nchini Sweden,hakuacha hata kitu kimoja,kila alichoambiwa na Sonia alikiweka wazi kwa Mume wake.Historia hiyo ilimfanya Mzee Santiago abaki kinywa wazi!
“Subiri,unamzungumzia huyu Sonia aliyefanya Wayte afilisiwe mali zake?”
Mr.Santiago akamkatisha Pendo,bado hakutaka kuamini kuwa mambo yamezunguka kiasi hicho.
“Ndiyo,mbali zaidi Sebastian ana Ukimwi”
“Niniiiiiii?”
“Subiri nimalizie”
Kila kitu kikawekwa wazi,mpaka anamaliza kuongea ilichukuwa kama dakika arobaini nzima.Mr.Santiago bado alibaki kimnya.
“Nachokuomba unishauri nini cha kufanya Santiago,Brenda atakufa.Naomba msaada wako,mimi nimeongea mpaka nimechoka”
“Nitajaribu kuongea naye!”
Mr.Santiago aliongea sentensi tatu peke yake kisha kuinuka,sura aliyoonesha ilimtia wasiwasi Pendo Jonas,sura yake iliweka makunyanzi.

****

Hakuwa mtoto wake wa kumzaa japokuwa alimpendal akini sio sana.Hata siku moja mzungu hawezi kujifananisha na muafrika hata iweje,atakuchekea usoni lakini moyoni ni tofauti kabisa.Jambo la Sebastian kuambukizwa ukimwi na Sonia lilimuuma kupita kiasi kwa kuwa tu alikuwa ni mtoto wa mzungu mwenzake,Waytte.
Waytte na Santiago walikuwa ni maswaiba wa kufa na kuzikana,walisaidiana kwa kila hali ndiyo maana walishirikiana katika mambo mengi tofautitofauti.
“Lazima nimueleze Waytte,siwezi kulifumbia hili swala macho hata kidogo.Hapana kwa kweli”
Siku hiyo jioni chumbani alijisemea na kuchukuwa mkonga wa simu,akabonyeza bonyeza namba anazojua yeye na kuruhusu simu itoke.
“Waytte,upo wapi?”
“Nipo chumbani kwangu”
“Naweza kuonana nawewe?”
“Sasa hivi?”
“Ndio sasa hivi”
“Sawa,wapi?”
“Twende kwenye mgahawa wa kahawa”
“Hakuna shaka”
Ilikuwa ni bora auweke wazi ukweli,kuliko kuendelea kuona familia ya rafiki yake inaangamia.Mr.Santiago akavaa viatu vyake na kushuka ngazi mpaka chini kwenye mgahawa wa hotel hiyo.
“Vipi hali Santiago?”
Mzee,Aidan Wayttte alianza kusalimia.
“Safi,acha nisizunguke zunguke.Kuna jambo nataka kukwambia”
“Jambo gani?”
Mr.Santiago akashindwa kuelewa ni wapi aanzie,alielewa habari alizotaka kutoa zingekuwa mbaya sana kwa rafiki yake.
***
“Darling, can you take me to my Aunt’s place?”(Mpenzi,unaweza kunipeleka kwa shangazi yangu)
“Now?”(Sasa hivi)
“Later on i think.Not now”(Baadaye nadhani,sio sasa)
“It's okay I’ll, i have no problem”(Sawa hakuna tatizo)
“I love you”
“Me too”
Sebastian na Brenda walikuwa katika maongezi ya kimahaba,wamekaliana huku wakimwagiana mabusu yasiyokuwa na idadi kamili,ndani chumbani kwao.Mapenzi kwa watu hawa wawili yalikuwa yamekolea.Waliyafurahia mapenzi yao ingawa hawakuwa na maelewano mazuri na Pendo Jonas,hilo hawakulijali sana.Ilimradi wanapendana na wana kila kitu katika maisha.
Pendo na mwanaye waliongea lakini hawakuwa na mawasiliano mazuri kama mtu na mwanaye,wakikutana husalimiana juujuu tu na kila mtu anaendelea na mambo yake.
“Wewe Brenda”
“Abee Mama”
“Unaenda saa ngapi kwa shangazi yako?”
“Nitaenda usiku”
“Usiku?”
“Ndio Mama”
“Utaenda na nani usiku?”
“Si na Seba”
“Lak…”
Pendo akashindwa kumalizia anachotaka kuongea,akabaki anamtizama mwanaye akimuonea huruma.
“Aya ukifika msalimie”
“Sawa Mama”
Hivyo ndivyo ilivyokuwa,ilibidi aache mambo kama yalivyo.
****
“Mimi nitaswali chumbani kwangu leo”
“Sawa,sisi tunaenda msikitini”
Ilikuwa ni usiku wa saa mbili,mida ya swala ya ‘insha’ watu wote walitoka na kumuacha Nasri peke yake,akidai kuwa ataswali chumbani kwake.Kumbe haikuwa hivyo,kichwani kwake alikuwa ana mahesabu yake makali,ilikuwa ni lazima amuingize Sonia chumbani kwake afanye naye ngono kwa dakika kumi,hakujuwa kuwa tayari ibilisi ameingia ndani ya mwili wake akiijaribu imani yake.
Alivyohakikisha watu wote wameondoka akachukuwa simu yake.
“Halloo Natasha,uko wapi?”
“Ndio nimefika hapa”
“Wapi?”
“Hapa chini,kwenye miti miti”
Nasri akakimbia haraka dirishani,akafungua dirisha akamuona Sonia kwa chini.
“Nimekuona nakuja”
Hakutaka kuamini kuwa ni kweli siku hiyo anaenda kumvua nguo ya ndani msichana mrembo kama huyo,tena kiulaini namna hiyo.Akashuka ngazi harakaharaka.
Mpaka kwenye miti,moyo wake ukapiga kwa nguvu sana,mwanamke aliyemuona mbele yake,alikuwa ni mzuri mno.Akili yake ikabadilika ikaanza kuwaza ngono tu.
“Mambo Natasha”
“Poa,wewe ndiye Nasri?”
“Ndio,njoo huku”
Nasri mbele Sonia nyuma,wakaanza kuongozana,mpaka wanapanda ngazi Nasri hakutaka kuamini, bado alikuwa akigeuza geuza shingo yake nyuma akimtizama Sonia.Wakati mwingine akili yake ilimtuma kuwa asingeweza kumfanya chochote maana katika maisha yake,hakuwahi kukutana na mwanamke mzuri kama huyo potelea mbali kuona nguo yake ya ndani.
Sonia alitingisha kwa uzuri.Alivyoingia chumbani kwake,akafunga mlango.
Akaanza kutetemeka mwenyewe na kubaki kimnya.
“Vipi?”
Sonia akavunja ukimnya.
“Hakuna kitu,wewe ndiyo Natasha?”
Nasri,akajikuta ameuliza bila kutarajia.Alijikuta ameishiwa maneno.Sonia alishaelewa,mwenyewe akasimama na kumuendea, akamfuata mdomoni na kutoa ulimi wake,akaupenyenza mdomoni mwa Nasri wakaanza kulana denda.
****
“Sijui tumepotea,sijui ndiyo hapa.Nashindwa kuelewa”
“Sasa si upige simu”
“Hazipokelewi”
“Kwani wewe hupakumbuki?”
“Hapa ndiyo Keko magorofani,lakini pamebadilika”
Marecedez Benz kibanda wazi,ilikuwa nje.Pembeni ya magorofa ya keko.Brenda na Sebastian walikuwa ndani hawakuwa na uhakika kama wamepotea au la!
“Griii griiiii”
Simu ndiyo iliwashtua.
“Ndiyo anapiga”
Brenda akaiweka sikioni,baada ya kupokea.
“Eh Brenda,mmefika wapi?”
“Ndio tupo magorofani sasa sijui ndiyo hapaaa shangazi”
“Mmefika ndiyo hapo,tulikuwa msikitini.Tupo njiani tunakuja”
Hazikupita dakika tano,walionana na kusahabiana kwa furaha,ni miaka mingi sana ilipita,kila mtu alionesha furaha.
Wakati shangwe zinaendelea yeye Sebastian alikuwa kimnya,hakuelewa lugha la Kiswahili,ndiyo maana akatulia hakutaka kushoboka.
“Huyu ni mpenzi wangu,anaitwa Seba.Hajui Kiswahili ni Mmarekani”
“Hapo ndiyo shughuli ipo,Shangazi yako sijui kiingereza.Ndiyo wanasalimia vipi?”
“Mwambie tu,Good everning.Inatosha”
Walikuwa bado wapo nje,Shangazi akakusanya pumzi ndefu ili kutoa salamu.
“Good everning”(Za jioni)
“Oh! Goodeverning to you”
Sebastian akajifanya kushtuka,wakapeana mikono na kuingia ndani.
“Hivi,Nasri yupo wapi jamani,nilikuwa nachat naye kipindi nipo Marekani.Amekuwa mkaka huyo”
“Yupo,yupo ndani.Tulimuacha ana swali ndani”
“Natamani kumuona”
“Twendeni ndani jamani,karibuni”
Kikundi kizima kikaongozana,Sebastian alikua ana kazi ya kushangaa huku na kule,aliyaangalia mazingizra ya uswazi kwa dharau.
Wote wakaingia mpaka ndani kila mmoja akapewa kikombe cha uji wa pilipili.
“Nasriiii,wewe Nasriii”
Shangazi aliita huku akitembea,mlango wa chumba cha Nasri ulikuwa hapohapo Seblen.Kitendo cha kufungua mlango kungemaanisha kila kitu kuonekana.Mbali na hapo kila mtu alipiga jicho lake kwenye mlango,hata sebastian nayeye alijikuta anautizama mlango.

***
Mzee Mfaume alikuwa ni tajiri mkubwa jijini Dar es saalam,hata katika orodha ya watu wenye pesa jina lake lilikuwepo,hakuwa na shida yoyote ile.Alisafiri kila mwisho wa mwezi na familia yake.Watanzania wengi walijuwa kuwa anaenda kufanya matanuzi tu.Kumbe haikuwa hivyo,siri ya kusafiri kila mwisho wa mwezi aliijua yeye na familia yake tu kuwa wanaenda kubadilisha damu.
Kwa jinsi alivyonawiri ungeambiwa kuwa ana virusi vya ukimwi ungebisha,Marafiki zake wengi walikuwa ni viongozi serikalini na walimshawishi aweze kuingia kwenye siasa lakini hakutaka, kwani haikuwa damuni,biashara zake zilikuwa siku hadi siku.Mbali na kuwa mfanyabiashara mkubwa, Mzee Mfaume alikuwa mkwepa kodi,aliijuwa sana pesa ndiyo maana alikwepa kodi.Alimwaga pesa bandarini ili makontena yake ya biashara yapite bila kutozwa ushuru,na ndiyo maana alipata faida kubwa katika biashara zake.Aliipenda sana familia yake,sanasana mtoto wake aliyekuwa mmoja tu aliyeitwa, Samia.
“Haya makontena yako wapi?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Johnson Mpeka na aliingia bandarini kwa kushtukiza,Wafanyakazi waligongana vikumbo.Ulikuwa ni mwezi mmoja tu tangu aapishwe kuwa raisi.
“Haya makontena Muheshimiwa,bado bado nadhani mafaili yake”
Mfanyakazi wa bandari alijikanyaga,hakujua ni kitu gani anakiongea.
“Nakuuriza tena,haya makontena yako wapi,yamepita bira kuripiwa ushuru?”
Raisi akazidi kuuliza,walinzi walikuwa pembeni yake, waandishi wa habari kazi yao ikawa ni kupiga picha.
“Mkuu wako wa kazi yuko wapi?”
“Hajafika Muheshimiwa”
“Tangu lini?”
“Tangu juzi”
“Alitoa taarifa?”
“Hapana,Ndio bosi ndio Muheshimwa”
“Nyie ndiyo watu tunawataka,naomba unieleze makontena hayo mia tatu yamekwenda wapi?na nina omba orodha ya wote wenye makontena yao tangu miaka kumi iliyopita.Nakupa dakika kumi”
Yalikuwa ni maagizo yaliyomchanganya Peter,isingekuwa kubana miguu yake mkojo ungemtoka.Hakudhani kama mambo yangebadilika kiasi hicho.Muheshimiwa Raisi akazidi kutembea na kukagua bandari.Hazikupita hata dakika ishirini majina ya wafanyabiashara wakubwa mia nane yalikuwa makao makuu ofisi za ‘Tanzania Revenue Authority’(TRA) yanakaguliwa.Karibia nusu ya wafanyabiashara walikuwa wakwepa kodi,akiwemo Mzee Mfaume.Hapo ndipo Raisi Johnson Mpeka alipokasirika.
“Hawa watu nataka watafutwe mara moja makontena zaidi ya mia tatu hayaonekani,washaifanya hii nchi ni shamba la bibi.Wataripa kodi na nitaendelea kuwatumbua”
Raisi Johnson aliongea siku hiyo kwenye moja ya hotuba zake,raia walimshangilia na ndiyo ilivyokuwa.
**
Mzee Mfaume alichunguzwa, mali zake zote zikashikiliwa, akaunti zake zikafungwa,hakuruhusiwa kuchota pesa yoyote ile.Mbali na hapo Passport yake ilishikiliwa kwa maana kwamba hakuruhusiwa kusafiri kwenda nchi yoyote ile mpaka uchunguzi ufanyike,hakuna siku ambayo hatokuja kuisahau katika maisha yake kama alivyoambiwa kuwa ana deni la shilingi tilioni saba,presha ilimpanda akadondoka puu chini,akazirai.
Alivyozinduka alijikuta hospitalini.Hakuna mtu aliyemuonea huruma,serikali ikashikilia mali zake na nyumba zake zikapigwa mnada,akaunti zake zikafilisiwa,akabaki hana kitu.
Kufumba na kufumbua dunia ikawa imempa kisogo,akawa ana hali mbaya maskini wa kutupwa,Ili kukimbia aibu yeye na familia yake wakakimbilia mkoani Tanga kujificha.Kutokana na kutokuwa na pesa za kusafiri kwenda kubadilisha damu ikafanya waanze kudhoofika,kiafya.
“Sina ujanja Mke wangu”
“Sasa itakuwaje?”
“Tusubiri tu miujiza ya Mungu”
Mtu na Mke wake walipeana moyo!
***
Habari za kufilisiwa mali za Mzee Mfaume zilivuma kama upepo,kila mtu alizijua.Samia alilia machozi maringo yote yakamwisha,akawa analia kila siku,hata siku moja hakuwahi kufikiria kuwa angekuja kuishi maisha ya kijijini,alishazoea asubuhi kuletewa chai nzito tena ya kizungu yenye kila kitu,alishazoea kula mlo kamili na kusafiri kila anapotaka kwenda.Hakutaka kuamini kuwa mambo yameenda kinyume.Kutokana na msongo wa mawazo mwili wake uliisha,alijisikia aibu wala hakutaka mawasiliano na mtu yoyote yule,akafuta akaunti zake zote Facebook na Instagram.Hakuna mtu yoyote aliyejuwa familia ya Mzee Mfaume ilipo.
‘LAKINI INABIDI NIMTAFUTE PARTSON,NIMWAMBIE UKWELI KABLA SIJAFA’
Aliamini kuwa siku zake za kuishi zinakaribia,baada ya kujiangalia kwenye kioo.
Hakutaka kufa bila kumwambia Partson ukweli juu ya afya yake kuwa ni muathirika wa Ukimwi, alielewa ni kiasi gani Mwanaume huyo ataumia moyo,mbali na hapo alikuwa anategemewa kitaifa.Hapo ndipo alipochukuwa simu na kumtafuta hewani.
“Halloo nani?”
Upande wa pili wa simu ulisikika,Partson aliuliza.
“wewe ni Partson?”
“Ndio, wewe ni nani?”
“Mimi Samia”
“Samia?Samia Mfaume?”
“Ndio”
“Mambo”
Jinsi Partson alivyosalimia,haikuwa kawaida.Hawakuwasiliana kwa takribani miezi saba.Hiyo ndiyo ikamfanya Samia aumie mtima.
“Poa,upo wapi?”
“Nipo Dar,vipi kwani?alafu kwanza pole kwa matatizo”
“Ahsante nishapoa,nawewe pole pia”
“Ahsante,mbona unanipa pole?”
Moyo wake ukawa mgumu kuongea lakini hakuwa na jinsi yoyote ile,ilibidi ukweli uzungumzwe japokuwa aliamini kwamba angeumia.
“Partson,naomba unisamehee sina jinsi zaidi ya kukwambia ukweli”
“Ukweli gani?Au unataka kuniacha kama unanipa pole ya kuniacha umechelewa Samia.Sasa hivi nina maisha yangu,samahani kwa kuchelewa kukwambia,nina mwanamke mwingine”
Partson bado hakujua ni kitu gani,akajifanya kumuwahi Samia ili asionekane kuwa amepigwa kibuti.
“Sio hivyo,Partson Mimi ni muathirika wa Ugonjwa wa Ukimwi,naomba unisamehee sikukuambia kabla.Naomba unisamehe”
Partson alihisi amepigwa na ganzi mwili mzima,aliganda.
Mapigo yake ya moyo yakapiga kwa nguvu akahisi kama uti wake wa mgongo umepigwa na shoti,akabaki ameduwaa.
“Partson unanisikiliza,huo ndiyo ukweli.Naomba nikutakie maisha mema”
Samia akakata simu!

***
“No Santiago,this is insane”(Hapana Santiago,huu ni upuuzi)
Sura ya Aidan Waytte,ilianza kujikunja.Baada ya kusikiliza kila kitu alichoambiwa na rafiki yake,moyo wake ulimuuma kama nini!hakutaka kukubali hata yeye kama mambo yangezunguka kiasi hicho.Habari za Sonia zilimuumiza moyo,mbali na hapo habari za ugonjwa wa Ukimwi ndiyo zikamuogopesha zaidi.
Ugonjwa huo aliuogopa kuliko ukoma.Kila alipozidi kumwangalia Santiago ndipo alipozidi kupandisha hasira.
“You have to calm down”(Punguza jazba)
“You are telling me to calm down?He is my son remember,My only son”(Unaniambia nipunguze Jazba,ni mwanangu)
Mzee Santiago aliongea na kupiga meza,vikombe vya kahawa vikadondoka,wateja waliokuwa pembeni wakawashangaa.
“I understand”(Naelewa)
“Then what?what if i was the one who telling you this, could you do what you asked me to do?Where is Pendo?”(Kwahiyo,ningekuwa mimi nakueleza haya,ungefanya kitu unachoniambia nifanye,Pendo yuko wapi)
“Waytte”
“Where is Pendo?”(Pendo yuko wapi)
“Listen to me Waytte”(Nisikilize Waytte)
Hakukuwa tena na maelewano hata kidogo,Mzee Waytte alivurugwa mno.Santiago katika maisha yake hakuwahi kumuona rafiki yake akiwa amekasirika kiasi hicho,alianza kujuta ni kiherehere gani kilimtuma aongee vitu kama hivyo,alijua tayari keshachochea vita.
“If my son is inffected you gona Suffer,trust me!”
Waytte aliongea kwa hasira na kusimama,macho yake yalimbadilika rangi.
Mwili mzima ukawa unamtetemeka kwa hasira,hasira zake zilikuwa waziwazi.Akatoka na kuingia ndani ambapo moja kwa moja alizama chumbani kwa Santiago,hakujali baada ya kumkuta Pendo anavaa yupo na chupi peke yake.
“What is the meaning of this?”
Pendo bado alikuwa na hasira,ndiyo maana akauliza kwa jazba alivyomuona Mr.Waytte ameingia chumbani bila kugonga mlango.
“Unajua kwanini nipo hapa,nachokwambia ni hivi.Kama mmepanga na mwanao mtajuta,nawaambia mtajuta.Kama mwanangu ana virusi vya Ukimwi nitaanzisha vita nawewe,kufa au kupona.Nife mimi au mfe nyie”
Yalikuwa ni maneno ya kuogopesha mno kwa Pendo,kwa mara ya kwanza hakuelewa ni kitu gani kilimaanishwa,akabaki anamtizama Mzee Waytte ambaye aliongea na kutoa lugha chafu,ikataka vita ianze,dalili zilionesha ni kweli mambo anayoongea Waytte, yanatoka moyoni mwake.
***
Walipigana madenda kitandani,Nasri akiwa juu huku mashine yake ikiwa ndani ya mgodi wa Sonia, wapo uchi wa mnyama wanafanya tendo lililowaleta duniani.Kutokana na mambo yalivyoenda harakaharaka Nasri alifika mshindo kabla ya Sonia,akabaki akihema kijasho chembamba kinamtoka,alijihisi ni mwanaume lakini ndani ya moyo wa Sonia alimdharau.
“Hana kitu kumbe,any way sio swala langu kazi yangu nishaifanya tayari”
Aliwaza Sonia akiwa chini ya Nasri.
“Baby nani kakufundisha haya mambo yote?”
Lilikuwa ni swali la kinafki kutoka kwa Sonia.
“Sio mtu mpenzi”
“Unajua sana kucheza,una demu?”
“Ndi..o hapana sina,tuliachana”
“Nakupenda Nasri.Naomba unipende kama ninavyokupenda”
Hivyo ndivyo Sonia alivyokuwa anamwambia Nasri kimahaba,kwa jinsi picha lilivyoenda haikuwezakana hata kidogo kwa Nasri kugundua kuwa hilo ni changa la macho!Na Sonia yupo hapo kumpa gonjwa hatari la Ukimwi.
“Natasha”
“Abee”
“Nakupenda sana”
“Ha..”
Kabla ya kumalizia Sentensi walisikia vishindo vya watu.Kwa Nasri alishaelewa tayari shangazi zake wameshatoka kuswali msikitini.
Hivyo wapo seblen.Kabla ya kujihami akasikia anaitwa jina lake.
“Natasha,njoo huku ujifiche”
“Unasema?nini?”
“Njoo njoo njoo”
Kama Umeme Sonia akavutwa na kupewa nguo zake,kwa kasi ya umeme akaanza kuzivaa.Bahati mbaya ilikuwa kwake,baada ya kuvaa tu nguo mlango ukafunguliwa.Wakaonekana wote waziwazi.
“Soniaaa”
Sebastian alikema na kugandisha kikombe cha uji,akamtizama Sonia na kutoamini kama ni kweli au anaota ndoto.
“Soniaaaa”
Akasema tena na kusimama kwa gadhabu,watu wote nyumbani hapo walipigwa na bumbuazi.Brenda akayatoa macho yake,akashindwa kuelewa kitu anachokiona kama ni cha ukweli.
Nguvu za miguu zilimushia Sonia akashindwa kuongea akabaki ameganda kama barafu,hakuelewa Sebastian amefikaje mahali hapo,alibaki akitetemeka mno.
“You Bitch”(Wewe Malaya)
Sebastian aliwapangua watu na kuingia chumba alichokuwa Sonia,bado alikuwa na hasira na mwanamke huyo.Sebastian siku zote alikuwa ni mtu mwenye hasira,alitetemeka na kumsogelea huku akiwa amekunja ngumi,kabla ya kuuliza chochote alimtandika ngumi ya usoni.
Hakuna mtu aliyeelewa ugomvi huo isipokuwa Brenda peke yake,dakika mbili zilizofuata hakuna mtu aliyeweza kumuelewa mwemzake,Sebastian alikuwa akitukana matusi kwa kiingereza cha kumung’unya.
Sonia alipigwa makofi yasiyo kuwa na idadi kamili.Nasri alivyoona hivyo akaingilia ili kumuokoa Sonia, lakini alipigwa ngumi ya pua akatulia pembeni.
“Sonia,i’m gona kill you right here,right now”(Sonia,ninakuuwa sasa hivi)
Sebastian aliendelea kutembeza kichapo kwa Sonia bila kujali,damu nyingi zilianza kumtoka Sonia puani na mdomoni,alipigwa mateke na ngumi.
Nasri alikuwa chini anaugulia maumivu ameshika pua yake damu nyingi zinamtoka kama maji bombani,akashikwa na hasira zaidi,akaangalia pembeni na kuchukua kikombe cha Uji,akampiga nacho Sebastian Kichwani kwenye utosi,Sebastian alidondoka chini na kuanza kutoa mapovu mdomoni,kila mtu alikuwa kimya.Hali hiyo ilifanya kila mtu aogope,dalili zilionesha kuwa Sebastian anakata roho!


****
Ilikuwa ni maiti iliyowachanganya askari,sime yenye makali kotekote ilikuwa imetumbukia tumboni mwa maiti iliyolala kandokando ya fukwe za bahari ya Hindi,Msasani beach.Hali ya sintofahamu ilitanda kwa wakazi wa eneo hilo asubuhi.Maiti ilipigwa picha na baada ya kupekuliwa na kuona vitambulisho kwa uangalifu waligundua anaitwa Julius Ikanza,mkurugenzi wa shirika la Umeme Tanesco.Hakuna mtu aliyejua chanzo cha umauti kumkuta isipokuwa Polisi ambao walimuweka chini ya ulinzi Gingi,mlinzi wake.
“Huyo maelezo atayatoa kituoni”
Ilikuwa ni kauli iliyotoka kwa Kamishna wa polisi wilaya ya Temeke, Afande Richard Urassa.Deffender zilikuwa kandokando ya maiti.Picha ziliendelea kupigwa za ushahidi,kila kitu kilivyokamilika maiti ya Julias Ikanza ikachukuliwa kwa ajili ya uchunguzi wa kina.
Gingi hakuwa na sababu ya kuficha jambo lolote ndani ya kifua chake,kila kitu alikiweka bayana!
“Nyuma ya haya kuna mapenzi kumbe?”
“Ndio afande”
“Marehemu alitaka kuzikata nyeti za huyo kijana?”
“Ndio afande,kama nilivyokwambia Mke wake akamsukumiza, sime aliyoshika ikamchoma tumboni”
“Mh,hii kali ya mwaka.Afande Oza embu njoo usikilize.Hizi kesi za mapenzi sijui zitaisha lini”
Matukio kama hayo kituo cha Kawe,yalifululiza,Gingi alitoa maelezo yake kila kitu kilivyoenda mpaka akapigwa na gongo kichwani.Kazi ya jeshi la polisi ikawa ni kuandika.
“Afande Maria”
“Abee”
“Utaongozana na Deffender ya Dulla,muende nyumbani kwa Marehemu mkachunguze”
“Sawa Afande”
Kauli hiyo ilitekelezwa mara moja,gari moja la polisi likawashwa na aliyewaongoza ni Gingi kufika nyumbani kwa Marehemu Julius Ikanza,waliamini kuwa watapata chochote kile cha kuanzia.Ni kweli walivyofika walijuwa kuwa hakuna mtu yoyote ndani ya nyumba hiyo,hata walivyoangalia makabatini baadhi ya nguo hazikuwepo.
“Inaelekea huyu mwanamke amekimbia,hayupo hapa”
Afande Maria alitoa taarifa akitumia redio upepo,ambapo Kamishna Richard Urassa alisikiliza na kutoa jibu.
“Hayupo! kwahiyo?”
“Naona vitu haviko sawa,nguo zimetupwa tupwa.Embu subiri afande naona picha hapa chini”
“Picha ya nani?”
“Kijana mweupe ana nywelenywele”
“Umeikuta wapi?”
“Hapa chumbani”
“Atakuwa ndiyo huyo Leythan,inawezekana kabisa.Embu muulize Gingi kama ndiye mweyewe”
Afande Maria akatoka nje na picha mkononi mpaka ndani ya defender,akaitoa na kumkabidhi Gingi.
“Huyu ndiye huyo Leythan?”
“Ndio,ndiye yeye”
“Unapafahamu kwake?”
“Kwa kweli hapana”
Leythan waliamini ndiye atakuwa msaada kwa jeshi la polisi ili kumkamata Conie,alidaiwa kumuuwa mume wake na kutokomea kusikojulikana.Hakuna kilichofanyika zaidi ya kuwatafuta ndugu wa marehemu ili wawaambie kila kitu kilichotokea,walisikitika sana na kulia machozi.
Lakini hata wao walimtaka mwanamke huyo ashikiliwe mara moja,walikuwa na polisi bega kwa bega ili wajue nini hatma na mwisho wa siku.
Leythan Jabir alikuwa akiswaka kila kona ya jiji la Dar es salaam,jeshi la polisi liliamini kuwa wangempata mtu huyo angewaeleza ni wapi Conie alipo,hakuna hata askari mmoja aliyekuwa na wazo kuwa mtu huyo yupo nchini Kenya,Mombasa ana kula raha,walizidi kumwaga maaskari kila kona, picha za Leythan zikasambaa chini kwa chini.Askari walifanya siri kubwa wakiamini kuwa wenda akigundua atakimbia na watakosa pa kuanzia.
“Huyu Leythan namfahamu ni Bwana ake Amina”
Mwanamke mmoja aliropoka siku hiyo maeneo ya Mtoni kwa Aziz ali.
“Una uhakika?”
“Ndiyo,Leythan huyu”
“Hapo kwa Amina unapafahamu?”
“Ndio,Amina anaishi Buguruni”
“Embu ingia ndani ya gari utupeleke,ulisema unaitwa nani?”
“Mimi naitwa Mwajuma”
“Mwajuma ingia ndani ya gari”
“Nimeinjika maharage jikoni,yataungua”
“Kazime jiko,kama kuhusu kula utakula huko huko”
“Sawa,nakuja sasa hivi”
Taarifa hiyo ilikuwa ni nzuri kwa jeshi la polisi,Mwajuma alikuwa amewapa mwanga mwingine kwani walimtafuta Leythan kwa takriban wiki tatu bila kumpata.
Mwajuma akafika, akaingia ndani ya gari la askari,Corrola.Hiyo ndiyo waliyoamua kutumia askari kanzu,hawakuvaa nguo za kipolisi japokuwa walikuwa mapolisi.
Kazi ya Mwajuma ilikuwa ni kuwaelekeza Polisi,’kata huku,nyoosha pinda kulia’.Mpaka walipofika Buguruni Rozana, wakakunja kushoto,wakaingia kulia gari likanyoosha mpaka nje nyumba yenye bomba la maji.
Mwajuma akawa wa kwanza kushuka na kwenda kuligonga geti na ndivyo alivyoambiwa na askari afanye hivyo.
“Hodi humu”
“Karibu”
Mwanamke aliyevaa kanga akatokeza.
“Mwajuma,ni wewe?”
“Ndio,za masiku shoga angu?”
“Safi shosti,umenitupa shoga angu.Kwanini unafanya hivyo,nina umbea huoo,we acha tu.Uniambie mbona umepotea kwanza?”
“Maisha tu”
“Karibu ndani,mbona kama upo mbiombio”
“Nina haraka,nina muulizia Leythan”
“Leythan!?”
“Ndio,Leythan nitampata wapi?”
“wewe wa nini? mbona wanitisha”
Maongezi yalivyozidi ilibidi mmoja wa askari ashuke,waliona ni kama wanachoreshwa na kupotezewa muda,hawakutaka stori nyingi walichotaka ni kujua ni wapi Leythan Jabir alipo ili wampate Conie.
“Habari,Mimi naitwa Afande Mutukuzi,tuna muulizia Leythan kama yupo ndani tuambie, kama hayupo tuambie tutampata wapi”
Amina alianza kutetemeka aliogopa sana askari.
“Usiogope”
Afande Mutukuzi akamtoa wasiwasi.
“Leythan,sijui yuko wapi kwa kweli,tuliachana muda sana”
“Una uhakika?”
“Sina sababu ya kukudanganya”
“Tukimkuta ndani je?”
“Hayupo, siwezi kuwadanganya nimesema, ingieni mkague”
Askari hakutaka kuamini alichoambiwa,akazama ndani na kuanza kumtafuta Leythan.
“Unapajua kwake?”
Aliuliza baada ya kumkosa ndani.
“Hapana kwa kweli,huwa tunakutana gesti house”
“Una namba zake za simu?”
“Ndio lakini hazipatikani”
“Mlikutana wapi siku ya kwanza?”
Polisi alianza usaili hapohapo.
“Nilipewa tu namba?”
“Mlikutana wapi?binti embu acha kujibu jibu ujinga.Usitupotezee muda.Ulipewa namba ndiyo nini?Mlikutana wapi?”
Polisi alifoka kwa ukali.
“Afande nilipewa namba na rafiki yangu tu”
“Rafiki yako gani?”
“Anaitwa Ashura,ndiyo nikakutana na Leythan”
“Huyo Ashura yuko wapi?”
“Mtaa wa nyuma,wala hakai mbali.Nitawapeleka”
Kazi ya kumtafuta Ashura ikaanza hapohapo,gari likageuzwa.Dakika mbili baadaye walikuwa Buguruni Sokoni,wakaipita baa ya sewa wakazidi kuingia ndani ndani.
“Simama hapa,yule pale”
“Yuko wapi?”
“Yule aliyevaa tshirt ya pink”
Kilichofanyika ni Ashura kuitwa na kuhojiwa maswali,ambayo majibu yake hayakueleweka vizuri.
“Unasema nawewe ulipewa namba?”
“Ndio afande”
“Nyie wanawake,msituchanganye embu twendeni kituoni.Mshaona sisi watoto”
Ashura,Amina pamoja na Mwajuma waliwekwa chini ya ulinzi.Safari ya kwenda kituoni ikaanza.
“Afande mimi mnanionea,naomba nimpigie simu kaka yangu.Niongee naye kwanza ajue kuwa nip..”
“Kaa kimnya,simbilisi wewe”
Walivyofika kituoni walikumbana na maswali mia moja kidogo, kila mtu kwa wakati wake,mpaka inafika jioni,polisi walifanikiwa kupata jina la Juma anayeishi Mabibo,usiku huo huo askari waliwasha gari mpaka Mabibo mwisho, nyumba namba 12K.
Wakagonga hodi.
“Mama shikamoo”
Askari alimsalimia Mama aliyetokeza mlangoni,Mnene kiasi mwenye mwili mkubwa.
“Mimi naitwa Afande Mtukuzi huyu mwenzangu anaitwa Kitundu,tuna muulizia Juma”
“Juma?”
“Ndio”
“Amefanya nini? mimi ndiyo Mama yake?”
“Tuna shida naye kidogo”
“Karibuni ndani”
Hapohapo Juma akaitwa,hakukuwa na muda wa kupoteza picha ya Leythan ikatolewa,wakitaka kujua alipo.
“Leythan huyu, nilisikia yupo Mombasa”
“Mombasa?”
“Ndio afande”
“Nani alikwambia?”
“Kuna jamaa mmoja hivi hapo saluni anaitwa Mchopa,ndiye kaniambia”
“Naomba tupeleke”
Mlolongo wa kumtafuta Leythan ulikuwa mrefu kama mkojo wa mlevi!
Askari walishaanza kuchoka lakini hawakukata tamaa,walifika kibanda cha saluni na kumuweka mchopa chini ya ulinzi.Hakuwa na sababu ya kukaa kimnya,aliongea kila kitu.
Tayari walishapata Muongozo wa Kumpata Leythan, wakiamini kuwa angewaonesha ni wapi Conie alipo,sababu walimtafuta kila sehemu wakamkosa,kila ndugu yake aliyeulizwa hakuwa na jibu ni wapi alipo Conie,hapo ndipo walipopata mashaka kuwa inawezekana akawepo na Leythan nchini Kenya, Mombasa.
“Sasa tutaenda au tufanye mawasiliano na askari wa Kenya?”
“Wawili wasafiri,huku tukiendelea kufanya mawasiliano na askari wa huko Mombasa”
“Unamjua yoyote kule?”
“Sio kitu kigumu”
“Mimi ninaijua Mombasa,A to Z”
Afande Maria akaingilia maongezi.
“Hapo itakuwa rahisi,inabidi uwende na Bosco Kesho msafiri”
“Hakuna shaka”
Mjadala ulivunjwa siku hiyo usiku wa saa tatu,Afande Maria na mwenzake ilibidi wapande basi kesho yake asubuhi,kuelekea Kenya Mombasa,ili kumkamata Leythan Jabir pamoja na Conie.

****
“Afande Kelly,upo wapi?”
“Nipo Limambo Grocery”
“Kuna mchongo nataka kukupa”
“Upi huo tena?”
“Inabidi tuongee face to face,ni wa pesa ndefu”
“Ndio uniambie”
“Nakuja Limambo Grocery hapo”
“Sawa,njoo utanikuta”
Maaskari wengi wa kituo cha Urafiki walipenda kunywa na kulewa katika ‘bar’ hiyo iliyokuwa maeneo ya Ubungo External,waliipenda sehemu hiyo sababu pembeni kulikuwa na wanawake wanaofanya biashara haramu ya kuuza miili yao,walilewa na kuondoka nao kufanya ngono, kisha kuwapa pesa kesho yake asubuhi au baada ya masaa kadhaa.
Na ndiyo maana hata mkuu wa kituo cha polisi Urafiki alipenda kujificha kwenye ‘bar’ hiyo pembeni kabisa kwenye kona.
“Psiii psiiiiii,weitaaa”
Afande Kelly alimuita muhudumu.
“Nikuongeze kinywaji?”
“Hapana naomba niite yule dada pale”
“Yule pale nje?”
“Ndio”
Afande Kelly aliitiwa dada poa aliyekuwa nje,akafika mpaka kwenye meza yake iliyokuwa gizani.
“Bei gani?”
“Show time buku tano”
“Sawa kaa hapo”
“Nipo kazini kaka,unataka mzigo tukamalizane”
Msichana mdogo aliyevaa kinguo kifupi alikuwa mbele ya afande Kelly,jinsi maziwa alivyoyapandisha na mapaja yake yalivyokuwa nje,haikuwa raisi kwa afande huyu mpenda ngono kuchomoka.
“Wapi sasa?”
“Kuna gesti huku nyuma,utatoa elfu tatu”
“Kwahiyo jumla Elfu nane?”
“Ndio”
Afande Kelly akasimama na kuongozana na Kahaba mpaka ndani ya gesti, ambapo alilazimika kulipia huduma ya gesti pamoja na kununua kondomu.
Wakaingia ndani akamkabidhi dada poa pesa yake.Harakaharaka akachojoa nguo zake,mashine yake ikiwa imesimama wima akavalishwa kondomu na dada poa, akajilaza chali akapandisha sketi yake juu,afande Kellly akampandia juu yake,hakukua na haja ya kuandaana, kazi ilikuwa ni kunjunju tu!
Na hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa afande,alianza kukatika huku akiwa ameishika miguu ya msichana huyu mdogo huku na kule.Hazikupita hata dakika tano,akawa tayari kamaliza anavaa nguo zake.
“Grii grii”
Simu yake,ikamshtua.
“Halloo,uko wapi?”
Upande wa pili ukauliza.
“Ushafika?”
Afande Kelly akajibu kwa swali.
“Ndio,nakutafuta sikuoni”
“Nipo nyuma huku navuta sigara,nisubiri hapo”
“Okay”
Afande Kelly alitaka kujua ni kitu gani anataka kuambiwa na afande mwenzake,akatoka haraka na kuzunguka.Akaingia baa,ni kweli alikutana na Afande Sagasa.
“Vipi Afande,mbona unanishtua?”
“Sio kukushtua,nataka kukupa mchongo wa pesa nyingi sana”
“Niambie sasa”
“Kuna mzee mmoja wa Kizungu,anataka kutoa milioni kumi kumi”
“Weee!”
Afande Kelly akayatoa macho yake kwa mshangao wa waziwazi.
“Ndio,ni hivi kuna binti anamtafuta”
“Enhee”
“Baada ya hapo sijui,lakini nadhani anataka kumuuwa kabisa”
“Wewe nani amekwambia?”
“Mackdonald”
“Embu fafanua vizuri nikuelewe, naona unaongea kama kasuku”
Taratibu Afande sagasa akatoa alichokuwa nacho ndani ya kifua chake,milioni kumi ilikuwa wazi endapo mpango huo utaenda vizuri.

****

“Embu kaa pembeni kwanza,apate hewa anatakiwa apate oxygen iingie kwenye mapafu,fungua mlango hewa iingie”
Sebastian alikuwa chini amelala chali anatoa mapovu mdomoni anapatiwa huduma ya kwanza,picha lilionesha kuwa anakata roho.
Ugomvi huo uliwashangaza sana watu waliokuwepo Seblen, kila mtu hakuelewa kivipi watu hao walifahamiana isipokuwa Brenda peke yake,lakini alikaa kimnya akajifanya hajui lolote.Sonia alivyoona hivyo alitoka mbio, hakutaka kuhojiwa maswali ya aina yoyote yale,alijua tayari Sebastian kapoteza maisha yake na kitu kama hicho kilishawahi kujitokeza miaka mingi iliyopita nchini Sweden baada ya kumpiga na chupa kichwani.

Hakuelewa ni kivipi Sebastian alitokeza eneo hilo,alichokifanya ni kutafuta bodaboda zilizokua nje zimepaki zinasubiri abiria.
“Mikocheni nipeleke kaka!”
“Mikocheni ipi?”
“Mikocheni B,shilingi ngapi?”
“Hapo kumi na tano”
“Poa twende”
Sonia akapanda nyuma,akiwa mwenye mashaka.Pikipiki ikaanza kuondoka huku kichwani akiwa na mawazo chungu mzima,alijua ni lazima Brenda ataropoka endapo Sebastian atakufa siku hiyo!
*****
Maaskari kumi walitembezewa pesa,kila mmoja alichukuwa shilingi milioni tano kama nusu ya malipo ya kazi iliyokuwa mbele yao ya kumtia Sonia mikononi ili wamuuwe kimnyakimnya,Mzee Wyatee alimchukia Sonia vibaya sana tangu akiwa nchini Marekani,habari za kwamba mwanaye kuna hatihati ya kuwa na ugonjwa wa Ukimwi ndizo zikamvuruga kupita kiasi! Ilibidi Sonia akamatwe na aliamini hilo lingefanyika masaa machache tu.
“Whaaaat?How?When?Where?Okay on my way”(Niniii,kivipi,lini,sawa nakuja)
Mzee waytte alipokea habari simuni iliyomshtua moyo kutoka kwa Mke wake Olivia akiwa hospitalini,Sebastian alikuwa na hali mbaya mno.Isingekuwa kuwahishwa hospitali ya Aghakhan wenda angepoteza maisha yake.
Habari hizo alizipokea akiwa ndani ya gari akitokea kituo cha polisi,ilibidi ampe dereva taxi simu ili aweze kuelezwa maana yeye alikuwa mgeni wa jiji hilo.
Ndani ya dakika arobaini alikuwa akitembea hatua mbilimbili kuingia wodini ambapo alifika mapokezi na kuongozwa moja kwa moja chumba kinachofuata,ni kweli Sebastian alikuwa akipumulia mashine ya hewa ya oksijeni kitandani.
Mke wake Olivia alivyomuona Mumewe alimkimbilia na kumkumbatia, akaanza kulia machozi.
“What hapenned?someone has to explain to me.Brenda start talking”(Nini kimetokea.naomba nielezwe,Brenda anza kuongea)
Hasira zake zote zilikuwa kwa Brenda,alimchukia sana kutokana na habari alizopewa.Na akili yake ilimtuma kuwa Brenda ndiye chanzo cha kila kitu ndiyo maana akamuuliza kwa sauti ya kufoka iliyojaa hasira,Sebastian alikuwa kila kitu kwake.
“Soni..a soo.niiaaa…”
Brenda akaanza kuongea,akamtaja Sonia.Na mbaya zaidi alisema kuwa ndiye amehusika na tukio zima,lililopelekea mpaka Sebastian awepo juu ya kitanda amelala.Hiyo ndiyo ikamfanya mzee Waytee apandwe na hasira zaidi na zaidi.
*****

Sonia alikuwa akiwindwa na maaskari sio akamatwe, bali auwawe kwa kupigwa hata risasi ya kichwa,haikuwa kazi ngumu kwa polisi kupajua Mikocheni B nyumba anayoishi Sonia Nickson Shayo,mikakati ilipangwa kuwa wamuingilie Usiku wamchukuwe kisha wampeleke Msituni Madale,huko ndipo wangempiga risasi na kuuchoma mwili wake moto ili kupoteza ushahidi.Wazo hilo lilitoka kwa Koplo Sadiki Makala na kila mtu akampongeza.
Usiku wa siku hiyohiyo waliweka Deffender yao nje ya geti kubwa,nyumbani kwa Sonia.
“Sasa nani ataingia?”
“Wewe Mkude ingia,sisi tutafuata.Uzuri hiyo nyumba anaishi peke yake,kwahiyo ondoa shaka”
“Kweli?”
“Ndiyo.Wewe ingia sisi tutafuata kama yupo tupigie simu au nitumie meseji.Lakini najua yupo, gari yake sindo ile pale nje”
“Ndio yenyewe”
“Basi ingia”
Maaskari walisemezana,Koplo Mkude akashuka ndani ya gari na kusukumiza geti ambalo lilikuwa limeegeshwa tu.Akatembea kwa mwendo wa hatua kama ishirini na saba ndiyo akaifikia nyumba ya Sonia,akagonga mlango.
“Wewe nani?”
Sauti ya Sonia ilisikika ikitokea ndani.
“Fungua,jirani yako”
“Unataka nini usiku wote huu?”
“Fungua mlango nikwambie jirani yangu”
Mlango ukafunguliwa Sonia akatoa shingo nje,kazi yake ikawa ni kumshangaa mwanaume huyo aliyedai ni jirani yake.
“Nikusaidie nini?”
“Hata karibu”
“Nitakukaribishaje wakati sikufahamu!”
“Ninaishi hapo mtaa wa nyuma,napita kila nyumba kutoa maagizo niliyopewa na mjumbe”
“Mbona muda umeenda,kwanini usingepita kesho asubuhi”
“Nilichelewa kutoka kazini,hata hivyo kesho nitaondoka asubuhi sana”
“Sawa pita ndani”
Angejua asingemkaribisha ndani,kazi ya Koplo Mkude ilikuwa ni kuchati na maaskari wenzake.Akawataarifu kuwa waingie Sonia yupo.
“Ujumbe gani huo?”
“Ni hivi hapa mtaani kun….”
Kabla ya kumalizia kitu kingine Koplo Mkude akachomoa bastola kiunoni mwake.
“Usipige aina yoyote ile ya kelele,tulia hivyo hivyo”
Moyo wa Soina ukapiga kwa nguvu,alitetemeka mno.Alibaki akiitizama bastola inayomwangalia.


 *****
Mapigo ya moyo ya Sonia yalikuwa yakipiga kwa nguvu na kutaka kutokeza nje ya kifua,hofu ya kifo ndiyo ilimtawala katika akili yake,hakuwahi kuiona bastola katika maisha yake aliishia kuiona kwenye filamu na jinsi inavyouwa vibaya sana endapo mtu huyo akiifyatua,vitu vikaanza kumiminika kichwani mwake akamkumbuka marehemu baba yake alivyoambiwa kuwa aliuwawa kwa kupigwa risasi hiyo ndiyo ikamfanya aogope zaidi.
Nguvu zikamwisha mwilini,miguu ikamtetemeka jasho likamtoka.
“Kaa chini!”
Kauli hiyo ilimshtua na kumfanya akae chini sakafuni bila kupenda,alihisi mkojo umem-bana lakini hakuelewa umetokea wapi.
“Tulia kama unaogeshwa”
Baada ya kauli hiyo tu,wakaingia watu wengine wanne ndani, wote walikuwa na bastola mikononi mwao.
“Sasa tunafanyaje?”
Mmoja akamuuliza mwenzake.
“Tuondoka naye,kama tulivyoongea au inakuwaje?”
“Ndio”
“Kelly yupo wapi?”
“Yeye kashafika,yupo Madale”
“Sawa,binti simama wima. Kabla hatujabadilisha maamuzi”
Watu hao ambao Sonia hakuwaelewa na kujua wametoka wapi walitoa kauli hiyo,bado hakuelewa ni kitu gani wanataka,ndiyo maana akaogopa hata kuongea chochote.
Akatembea taratibu kwa hofu mpaka nje,mawazo ya kukimbia ghafla yakamjia lakini nafsi nyingine ikamwambia asifanye hivyo sababu asingeweza kukimbia popote pale maana angeuwawa kwa kupigwa risasi, bado alihofia kufa.
Wote wakaingia ndani ya gari wakiwa na Sonia katikati,hapo ndipo alipomkumbuka Mungu na kusali sala ya ‘Baba yetu’ kimoyomoyo. Kifo ndicho alichoamini kinafuata muda mfupi tu,japo hakuelewa ni kwanini anaenda kuuliwa.Alijaribu kukitafakari kifo kinafanana vipi, akashindwa kupata jibu sahihi,alikiogopa kwasababu hakujua mtu akifa anaenda wapi,licha ya yote kwa dhambi alizofanya aliamini Jehanam inamuhusu,malaika wa adhabu wanamsubiri kwa hamu na moto wa shetani pia!

Ndani ya gari hakukuwa na mazungumzo yoyote yale zaidi ya watu hao aliyodhani ni majambazi kubonyeza bonyeza simu zao na kutabasamu.
“Kelly,ushafika?”
Mmoja wao alikuwa akiongea na simu.
“Ndio nimefika,mpo nae tayari?”
“Ndio”
“Sawa nawasubiri”
Maneno hayo yote Sonia aliyasikia na hakuelewa Kelly ni nani.
“Ka..ka”
Sonia akaita kwa uwoga wa waziwazi.Wote wakamgeukia.
“Nini?sema!”
Jinsi askari huyo alivyoyatoa macho yake ikamfanya Sonia aogope zaidi.
“Una lolote la mwisho la kusema?”
“Kwa..ni mnanipeleka wapi?”
“Utajua ukifika,lakini kama unataka kusali sala ya mwisho wewe Sali tu”
Yalikuwa ni maneno ya kutisha na kuogopesha moyo,Sonia akazidi kuogopa zaidi na zaidi.Moyo wake ukazidi kumdunda ndani kwa ndani.Maneno aliyoambiwa yakazidi kumpa majibu ya maswali yake,sababu alielewa nini maana ya kusali sala ya mwisho.
“Sa..sa kwanini mna..taka kuni..ua,nimefa..nya nini?”
“Wacha maswali kunguni wewe,au tukuuwe hapahapa?”
Ki ukweli hawakuwa na uwezo wa kumuuwa Sonia ndani ya gari,huo ulikuwa ni mkwara wa kumtuliza, Polisi walikuwa wana mikwara kupita maelezo yaliyojitosheleza,hiyo ndiyo ikamfanya Sonia aanze kulia machozi ya kwikwi,kifo cha kuuliwa kwa kupigwa risasi ndicho kilikuwa mbele yake kutokea,hakujitofautisha na Jogoo mkubwa wa ‘Christmass’ anayeenda kuchinjwa!
***
“Si nimekukataza kuvaa modo?”
“Ndio Madam”
“Sasa mbona umevaa?Nifuate ofisini”
“Lakini Mwalimu sina suruali nyingine”
“Kwahiyo?Mimi nikununulie au?”
“Hapana”
“Kumbe?”
“Nisamehe”
“Njoo ofisini,usinichefue nyie wanafunzi bila kupelekwa mputa hamuwezi,nifuate ofisini sitaki kusikia chochote kutoka kwako”
“Mwalimu Nasra”
“Abee”
“Huyo mwanafunzi ukimalizana naye mlete kwangu”
Ndani ya shule iliyoitwa St.Mathew’s Secondary school ndipo Nasra alipokuwa ameajiriwa kama mwalimu wa nidhamu baada ya kuhitimu masomo ya Chuo kikuu Mlimani,alifanya kazi kwa bidii zote na pesa alizopata kidogo alimtumia Mama yake, Rukia.Aliyekuwa mkoani Mwanza,alimpenda sana sababu ndiye aliyemuhangaikia mpaka akafika hapo alipo.
Alifundisha somo la Historia pamoja na Geography,uzuri aliokuwa nao ulifanya wanafunzi wa kiume wapende kuuzuria somo lake ili mradi tu wamuone Mwalimu Nasra, licha ya kukubalika lakini hakutaka mazoea yoyote yale na wanafunzi ndiyo maana kosa kidogo aliwachapa viboko.
“Sawa Mwalimu,wewe Happy,Ndio wewe kaniletee kiboko ofisini”
Mwanafunzi aliyekuwa pembeni aliacha anachofanya akakimbia ofisini kutafuta fimbo.
“Hiii ndiyo fimbo?Wewe Happy usinitanie.Leta fimbo kubwa”
Dakika moja baadaye fimbo ilikuwa mbele ya Mwalimu Nasra Shayo.
“Shika hapo,shika hapo Utali”
“Mwalimu”
“Shika hapo,usinipotezee wakati.Nimekwambia shika meza”
Mwalimu Nasra hakuwa na utani,bakora zilitembea makalioni mwa Utali hapohapo,tena zilimuingia na modo aliyokuwa ameivaa.Mwalimu Nasra akazidi kuogopeka.
Ratiba ya Nasra ilieleweka siku zote,kuwa saa kumi na moja anatoka shuleni na kusubiri ofisini ambapo anakuja kuchukuliwa na gari aina ya Mark x nyeusi,gari hiyo ilijulikana shule nzima,mbali na kujulikana hakuna hata mmoja aliyejuwa wala kutaka kuuliza kuhusu mwanaume anayekuja kumchukuwa mwalimu Nasra kumpeleka nyumbani,waliogopa kumuuliza.

Siku hiyo ilikuwa Ijumaa kama kawaida ya siku zote,siku hiyo haikuja gari aina ya Mark x kama walivyozoea, badala yake ilipaki Nissan Murano,hakuna mtu aliyejuwa ni gari ya nani,hata Nasra mwenyewe hakuwa na habari nayo.Mpaka aliposhuka mwanaume mrefu aliyejazia kifua,mweupe.
“Nasra,twende”
Hapo ndipo alipogundua kuwa ni gari ya mchumba wake Mustapha Masatu.Alijiuliza maswali mengi kuhusu gari hiyo mpya bila kupata jibu la swali lake.
“Ingia ndani ya gari”
Mustapha Masatu alisema baada ya kumuona Nasra ameduwaa.Wote wakaingia ndani ya gari lakini bado Nasra alikuwa ana mengi ya kuuliza.
“Vipi?”
“Gari,umetowa wapi?”
“Nimenunuwa love,isitoshe nimepandishwa cheo pia”
“Kweli?”
“Sasa hivi mimi ni Captain”
“Baaaaaby”
Ilikuwa ni shangwe kubwa,Nasra akashindwa kuzizuia hisia zake akamsogelea karibu Mustapha akatoa ulimi wake akautumbukiza kinywani kwa bwana ake,wakaanza kunyonyana ndimi!
“Baby twende nyumbani,okay?”
“Sawa love”
Gari ikawashwa,jinsi ilivyokuwa mpya hata kiyoyozi chake kilikuwa kina ubaridi mkali.
“Love”
Mustapha aliita baada ya gari kusimama kwenye foleni.
“Abee mpenzi”
“Fumba macho”
“Umeanza baby mambo yako,siku ile uliniambia nifumbe macho,nikafumba mpaka basi”
“Ha!Haa, baby fumba macho bwana”
Ni kweli Nasra alifumba macho,akahisi mkono wake wa kushoto unachukuliwa, kidole cha tatu kutoka mwanzo kuna kitu kinavikwa,jambo aliloliwaza kwa wakati huo hakuwa na uhakika nalo moja kwa moja,akasubiri mpaka aambiwe afunguwe macho.
“Fumbua macho yako”
Hakuamini macho yake,kama kidoleni mwake kuna pete,hata siku moja hakuamini kama Mustapha angekuja kumvalisha pete ya uchumba,alimchukulia ni mwanaume wa kupita tu kama wengine.Jinsi alivyoshangilia ilikuwa ni kama kaona goli limefungwa na timu anayoipenda!
“Bebiiiiiiiiiiiiiiii”
“Will you marry me, Nasra?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Mustapha.Ambalo jibu lake lilijibiwa ‘NDIO’ wote walikuwa wana furaha sana.
“Lakini love,kweli nitaweza?”
“Kwanini?”
“Kazi yako hiyo hatari,kila siku nipo roho juu juu”
“Naelewa,hilo usijali uzidi kuniombea”
Gari likatembezwa mpaka Mtoni kijichi alipopanga Nasra chumba chake,hakuna kilichoendelea hapo zaidi ya kuvuana nguo zao na kupigana mabusu.

Ndani ya dakika mbili kila mtu alikuwa kama alivyozaliwa,Nasra cha kwanza kukifanya ni kuushika Mwiko wa Mustapha na kuutumbukiza mdomoni,Mwanamke huyu aliujuwa mchezo huo balaa!alizidi kuyakusanya mate mdomoni na kufanya kama anauchuwa,Mustapha hakuwa na kauli zaidi ya kutulia tu kama mtoto mdogo anayeogeshwa,Nasra akazidi kufanya madoido na kuongeza njonjo!Kwa furaha aliyokuwa nayo siku hiyo ilibidi afanye kila jitihada ili kumuonesha Mustapha ufundi wote,alivyomaliza akaitoa koni mdomoni na kuanza kumlamba kifua, akasogea mpaka kwenye chuchu za Mustapha na kuanza kuzinyonya,hapo ndipo Mwanajeshi huyu aliyekuwa na cheo cha ‘captain’alipozidi kutoa mihemo ya ndani kwa ndani.Alihisi raha za ajabu,hata angetokea jambazi asingeweza kumfanya chochote kile.Nasra akazidi kumlamba kila mahali, akaingiza ncha ya ulimi wake sikioni,akamnyonya mpaka pua na macho baada ya hapo akampandia kwa juu,akaweka mwiko vizuri ndani ya kibakuli.Alivyohakikisha umeingia, akaanza kukinyonga kiuno chake taratibu huku akitoa miguno ya kimahaba.

*****
“Mpenzi”
“Naam”
“Nakupenda sana,ndoa lini Mpenzi wangu?”
“Nikirudi tu kutoka Comoro”
Nasra aliuliza maswali huku akiangalia kidole chake chenye pete,akiwa juu kifuani mwa Mustapha.
“Leo nataka tutoke”
“Twende wapi mpenzi?”
“Kuna sehemu hivi,nimeandaa special,utapaona.Kuna marafiki zangu huko nataka uwaone”
“Sawa,mimi sina tatizo”
“Sasa hivi,wananisubiri tukaoge”
Wote wakasimama,wakaingia kuoga na kurudi.Mustapha akachukuwa begi dogo lililokuwa na bastola yake ndogo,akachomoa ‘magazine’ ili kukagua kama ina risasi,alivyoridhika alirudisha na kuiweka kiunoni akaifunika na shati.
“Baby,mimi naogopa bastola ujue”
“Usiogope,hii ndiyo inanilinda.Ukitoka wewe huyu hapa”
“Ha!Haa!Haaaa! kwahiyo huyo ni mke mwenza wangu?”
“Ndiyo maana yake”
“Hivi baby ushawahi kuuwa mtu kwa bastola?”
“Kwanini unauliza,ndiyo nilishawahi”
“IIikuwaje?”
“Ilikuwa usiku siku hiyo napita,nikaona dereva wa pikipiki kapigwa anataka kuibiwa pikipiki yake,nikakoki bastola nikaua wale wezi”
“Mh! Inaelekea namimi utakuja kuniuwa eeh?”
“Siwezi”
Walitoka nje na kufunga mlango,walivyohakikisha kila kitu kipo sawa wakatembea mpaka walipoliacha gari.wakaingia na kuondoka.

Gari ilitembezwa kwa karibuni nusu saa nzima bila kufika,msongamano wa magari Ubungo ndiyo uliowafanya wachelewe.Walizidi kunyooka mpaka wakafika Tegeta, huko wakazidi kuingia ndani ndani.
“Baby tunaenda wapi?”
“Madale…aaah shit mpaka nimeropoka nilikuwa sitaki kukwambia”
“Macho yako”
“Kama yako,huko kuna kisiwa fulani nataka twende,pazuri sana”
“Usiku huu?”
“Kwani kesho unaenda kazini?”
“Hapana”
“Basi usijali”
Wakazidi kusonga mbele mpaka walipofika kwenye maegesho ya magari, hapo walilazimika kushuka na kutembea kwa miguu kuelekea kwenye kivuko kitakachowapeleka kisiwani.
“Baby mkojo umenibana”
Alisema Nasra na kuangalia pembeni ambapo kulikuwa kuna kichaka chenye miti mingi.
“Fanya haraka basi ili tuwahi”
“Ok”
***
Sonia alifikishwa katikati ya msitu uliopo Madale ili auliwe kwa kupigwa risasi kisha mwili wake uchomwe moto wakitumia mafuta ya petroli,Polisi hawakuwa na utu, pesa ndiyo iliyowapelekea watake kuuwa. Na kwa uzoefu waliokuwa nao waliamini kuwa hakuna mtu yoyote atakayejua ni wapi Sonia alipo,mipango ilipangwa kiakili mno.
“Mfunge na kamba,mweke pale nilenge shabaha.Afande nipe risasi moja.Hakuna kupoteza muda,nipe hiyo revolver”
Uhai wa Sonia ulikuwa mikononi mwa watu hawa ambao alidhani ni majambazi,bado aliendelea kulilia uhai wake, akafungwa na kamba na kusimamishwa mtini ili apigwe risasi moja ya kichwa tu.
“Dumu la petroli hili hapa”
Hiyo ndiyo ilimchanganya zaidi Sonia,taswira ya majivu ya mwili wake baada ya kuchomwa na moto vilianza kujijenga,akajiona jinsi atakavyogeuka na kuwa majivu,alihisi maumivu hata kabla ya kupigwa risasi.
“Muweke vizuri,mulika tochi hiyo usawa wa kichwa”
Afande Mbuya ndiye aliyekuwa na Rivolver mkononi akaiweka risasi na kumuangalia Sonia anayelia mbele yake,hakuwa na huruma hata kidogo alizifikiria pesa zilizobaki kama salio baada ya kumaliza kazi hiyo.
“Kaaaaa”
Mlio wa kipande cha mti kiliwashtua,wakamulika tochi zao,walihisi kuna mtu anawaona.Ni kweli walikuwa sahihi kila walichokifanya kilionekana na Nasra,bahati mbaya akakanyaga mti alivyotaka kuondoka taratibu.
Moyo wake ukaanza kupiga kwa nguvu,watu aliokuwa anawatizama walimwona akakimbia huku akimwita ‘MUSTAPHA’kwa sauti.
“Mustaphaaaaaa!”
Kabla ya kufika mbali risasi ilifyatuliwa,isingekuwa kuteleza kwa Nasra na kudondoka kifudifudi risasi ingekuwa imepita kisogoni mwake na kumuuwa hapohapo,Mungu ndiye alikuwa naye.
Kama umeme Mustapha akachomoa bastola yake kiuoni na kuikoki ili kuruhusu risasi zichomoke baada ya kusikia mlio wa bastola, akakimbia na kuingia msituni,alikuwa ni mwanajeshi na alielewa yupo katika hatari,hivyo alitakiwa kujihami.
“Nasraa,Nasraaa”
Mustapha aliita kwa sauti ya chini,huku akisogea taratibu ndani ya msitu uliokuwa na giza totoro.
Mwanajeshi huyu alijiamini kupita kiasi akaikamata bastola yake kwa mikono yake yote miwili, akatizama huku na kule.
“Weka bastola chini,kabla sijafumua hicho kichwa chako,fanya upesi”
Mustapha ndivyo alivyoambiwa,alihisi kitu kama kichuma kimemgusa kisogoni kumaanisha kuwa asalimu amri na kuweka bastola yake chini,akili yake ikawa inafanya kazi kwa kasi ya ajabu.Ikachambua mambo harakaharaka kama kompyuta isiyokuwa na mafaili.Akameza fundo la mate,hakuwa na uhakika na hatua anayotaka kuichukuwa,alielewa kuwa akiikosea tu huo ndiyo ungekuwa mwisho wa maisha yake siku hiyo.
Jambo alilokuwa anataka kulifanya lilikuwa ni sawa na kucheza kamali,kupata au kukosa.Taratibu alishusha mkono wake wenye bastola chini kumaanisha kusalimu amri,kwa kasi ya mwewe akarudisha kichwa chake nyuma,akajizungusha na kuupiga mkono wa mtu aliyekuwa nyuma yake,kabla hajakaa sawa akaruka teke lililotua kifuani mwa mtu aliyemshikia bastola,haraka akamsogelea.
“Paaaaaaaaaa”
Mlio ulisikika mkubwa wa bastola,maumivu aliyosikia Mustapha yalikuwa makubwa.Alikuwa chini anavuja damu mguuni,kapigwa risasi na mtu aliyetokeza nyuma yake.
“Kachakacha”
Askari akakoki bastola na kumuwekea Mustapha kichwani,hakuwa na ujanja mwingine wowote!

***
Maumivu aliyokuwa anayahisi mguuni mwake hayakuwa na mfano wake,damu nyingi zilimvuja, bastola yake ilikuwa kando.Risasi ilipenya mguuni mwake na kusababisha jeraha kubwa hiyo ilimfanya ashindwe hata kusimama na kujitetea.Akaburuzwa mpaka katikati ya msitu ambapo alimkuta Mpenzi wake Nasra nayeye amekalishwa chini na mwanamke mwingine ambaye hakumtambua kwa harakaharaka.
Sonia alizidi kuchanganyikiwa,hakuelewa watu walioletwa wametokea wapi,kutokana na mwanga hafifu akashindwa kuona vizuri nyuso zao.
“Inakuwaje?”
Jitu moja likamuuliza mwenzake baada ya kuwatizama.
“Tuwamalize tu,unadhani kuna cha ziada hapa”
“Poa”
Yakakubaliana,jambo la kuwaondosha Sonia,Mustapha na Nasra duniani kwa kuwapiga risasi ndilo jambo walilopanga kulifanya,waliogopa siri yao kuvuja,wote wakachukuliwa na kupangwa pembeni ili wauliwe mara moja,kila askari akashika bastola yake tayari kwa kufyatua risasi.
“Paaaaaa paaaaa paaaaaa”
Risasi zilisikika.
***
Mlio wa risasi iliyofyatuliwa ulisambaa sana,kutokana na Mustapha kukata mawasiliano baada ya mlio mkubwa wa bastola kusikika kulifanya wanajeshi waliokuwa kisiwani waingiwe na wasiwasi mkubwa sana.Kisiwani kulikuwa na wanajeshi kumi na mbili,wote walikuwa wamevaa nguo za kiraia wanasubiri sherehe ambayo Mustapha aliipanga kuifanya ndani ya kisiwa hicho.
“Bogere,sio mlio wa risasi huo”
M.P Magdalena John alimuuliza Mwenzake.
“Ndiyo,ni mlio wa risasi huo na Mustapha amekata simu”
“Yuko wapi kwani?”
“Upande wa pili kule,ndiyo alikuwa anataka kupanda boti”
“Nahisi kuna tatizo”
“Hamna bwana”
Wanajeshi walizidi kushauriana,hawakukaa sana wakasikia tena mlio wa bastola hapo ndipo hawakutaka kujiuliza, kila mtu alikimbia kuelekea kwenye boti ndogo waliokuja nayo.Akili zao zote ziliwatuma ni lazima mwenzao Mustapha atakuwa kwenye matatizo,boti iliwashwa injini ikaanza kuzunguka na kukata maji,kila mtu akaweka bastola yake vizuri mkononi.Boti ikazidi kusonga mbele, uzuri siku hiyo hakukuwa na mawimbi mazito,haikuwachukuwa muda sana wakaanza kuuona msitu wa madale, hata kabla boti haijashuka vizuri, Mp Magdalena akaruka majini na kuanza kukimbia, akaangalia huku na kule,alivyopiga jicho chini aliona hatua za viatu zimeelekea msituni, hapo ndipo alianza kuzifuata na kuzama msituni,akiwa na bastola yake mkononi kaishika vizuri.
“Paaaaaaa paaa paaaa”
Hakutaka kujiuliza mara mbili,alifyatua risasi zikawadondosha askari watatu chini,hapo ndipo ilipoanza vita.
Askari na wanajeshi walianza kutupiana risasi.Siku zote mwanajeshi hakufundishwa kupiga risasi mguuni bali alifundishwa kupiga risasi kifuani na kichwani na ndivyo walivyokuwa wakifanya wanajeshi hawa waliochukulia moja kwa moja watu hao ni majambazi.
Haikuwa kazi ngumu kwao, askari wote walikuwa chini wanavuja damu,wameuwawa!
“Mustapha..Mustaphaaa”
“Naaaam”
“Vipi?”
Hiyo ndiyo ilikuwa pona ya Sonia,isingekuwa hivyo wenda dakika hiyo angekuwa mfu.

****
Hakuna kitu kilichomfanya awaze kama siku hiyo alivyoambiwa na Samia kuwa ana virusi vya ukimwi,habari hizo zilikuwa tata kwake,alitamani kuijua afya yake lakini alishindwa kufanya hivyo kwani aliogopa mno,hakuelewa siku atakayopokea majibu kuwa ana virusi vya ukimwi angefanya nini.
Aliuogopa ugonjwa huo sababu uliuwa vibaya sana kabla ya kumtowesha binadamu duniani.
“Mimi sina ukimwi lakini mbona watu wanafanya mapenzi na wagonjwa wa Ukimwi lakini hawapati”
Partson alijifariji baada ya kupiga jicho lake kwenye kioo afya yake bado ilimridhisha,licha ya kujifariji lakini bado alikuwa mwenye wasiwasi kupita kiasi.
Mawazo ya kwamba ameathirika na ugonjwa wa ukimwi yalizidi kumtesa akakosa raha,kuna nafsi nyingine ilimtuma kuwa aende kupima ukimwi lakini nyingine iliogopa kufanya hivyo.Hayo yote yalikuwa yanapita kila kukicha,asubuhi,mchana na usiku!
“Darling vipi?Mbona nagonga mlango muda wote, kumbe upo ndani hata kuniambia”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Mwanamke mtu mzima mnene kiasi,kwa picha ya harakaharaka alionekana kumzidi umri yaani ‘sugar mamy’
“Devotha embu subiri, sipo sawa”
“Partson”
Mwanamke mtu mzima aliyefahamika kwa jina la Devotha,hakutaka kuelewa somo, alizidi kumsumbua partson akimfuata midomoni akitaka kumpiga denda lakini ilishindikana, Partson alikwepesha mdomo wake,kwa jinsi alivyokuwa na mawazo tendo alilotaka kufanyiwa muda mchache ujao halikuwa akilini mwake na kwa wakati huo aliwaza juu ya afya yake!
“Devotha,embu niache kwanza nina mawazo”
“Mawazo yako yanahusu nini?Mimi nina nyeg** tangu juzi nakupigia simu hupokei unadhani nitafanya nini?”
“Kwani huna mume?”
“Kale kazee mimi nitakapeleka wapi?hakawezi mambo ndiyo maana nipo hapa.Partson usinifanye niondoke hivi nikajitie vidole”
“Devotha,sipo katika mudi tafadhali nenda tu”
“Hapana Partson,mimi siwezi kuondoka”
“Unataka nini?”
“Hujui au makusudi”
“Najua sema,Ah!”
Devotha alikuwa ni mwanamke wa kikwere,alikuwa ni mtu mzima kiasi na mwenye watoto watatu,siku zote alikuwa ana shida kubwa sana ndani ya ndoa yake,alitamani kumpata mwanaume atakaye kidhi haja yake na kumfikisha mshindo.Tangu aolewe ndani ya ndoa yake yapata miaka sita hakuwahi kufaidi ndoa yake ingawa alikuwa anasikia kwa rafiki zake jinsi wanaume zao wanavyowaridhisha.
Siku aliyokutana na Partson ‘Club’ ndiyo hiyo siku alipojifanya kujilewesha na kujilegeza,alikuwa akijaribu kumpa penzi mwanaume huyo mcheza mpira akijaribu bahati yake kama anaweza kitandani.
Katika maisha yake siku hiyo ndiyo hakuweza kuisahau, alienda mshindo mizunguko minne kwa masaa kadhaa,raha alizohisi ndizo zikamfanya isiwe rahisi kuachana na Partson,hakuelewa lolote kuwa maisha yake tayari yapo hatarini kwa kupata ugonjwa wa Ukimwi.
“Sema nini tatizo?Umenichoka au?”
Devotha aliendelea kutoa sauti ya puani,Mungu alimjalia kumpa sauti ya kipekee na kalio kubwa,ngozi yake ilikuwa laini na alipewa pua nzuri iliyochongoka kama ya kitusi.Ungemuangalia harakaharaka usingedhani kuwa ni Mama mwenye watoto wakubwa.Alimsogelea Partson na kuanza kupapasa juu ya suruali yake taratibu akitafuta karoti ya Partson.
Ni kweli hakuwa na wazo la kufanya ngono kwa wakati huo bado alikuwa anaogelea kwenye bahari ya mawazo,aliufikiria ukimwi unavyotesa ndiyo maana hata mkono wa Devotha ulivyopita juu ya karoti yake aliutoa na kuzidi kutafakari, mambo mengi yalimiminika kichwani mwake akawa kama anaangalia filamu ya kihindi akajiona yupo ndani ya jeneza watanzania wanamlilia kiungo wao,akawaona wazazi wake wanavyolia machozi,mapigo yake ya moyo yakazidi kumwenda kasi.
Kwa mbali mawazo hayo yalianza kupotea baada ya kuanza kuhisi hali ya ujoto,alipoangalia vizuri akaona karoti yake imetolewa nje tayari na Devotha,hakuelewa imetolewa wakati gani.Mawazo aliyokuwa nayo taratibu yalianza kupotea, karoti yake ikaanza kutuna kisha kusimama wima,ghafla akamuona Devotha kaitumbukiza mdomoni anaichuwa taratibu.
Hapo ndipo damu yake ikaanza kumuenda kasi,akaanza kuhema ndani kwa ndani.Akazikamata nywele za Devotha vizuri na kuanza kukikandamiza kichwa chake vizuri ndani ya karoti yake.Akili yake ikahama mawazo ya ukimwi yakafunikwa tayari,alichokuwa anawaza wakati huo ni kuzini tu.
Akamvuta Devotha karibu na kuanza kupigana denda,wakaanza kuvuana nguo harakaharaka kama umeme,wakabaki kama walivyozaliwa, kwa jinsi mwanamke huyo alivyopenda ngono hakutaka tena jambo lingine lolote lile zaidi ya kuchukuwa karoti ya Partson na kuitumbukiza ndani ya mgodi wake,hapo ndipo alipoanza kuhisi raja zilizozidi kipimo,mishipa yake ya mwili yote ikamsimama akaanza kukinyonga kiuno chake huku wakipigana denda na Partson,akampindua Partson kisha kukaa juu yake,akazidi kukinyonga kiuno chake huku mikono yake akiwa ameiweka kitandani,kila alipozidisha kasi ndipo alipozidi kuhisi raha zinakuja.
Akazidi kukizungusha kiuno chake mpaka kitanda kikaanza kunesa na kutoa milio.
“Ah ah sshs aah aaaah! Part…so..n aaaaah!”
Huo ndiyo ulikuwa mwisho wa safari yake,alifika kitonga na kumlalia Partson kifuani mwake huku kijasho kwa mbali kikiwa kinamtoka!
***
Sonia alikuwa akilia machozi mfululizo tena bila breki, hakuamini kama amepona kwenye kifo cha kuuliwa na kuchomwa moto,wanajeshi wote walimuonea huruma.Kila walipojaribu kumuhoji walishindwa sababu ya kwikwi iliyom-bana.
“Binti,usilie unaitwa nani?”
Bado aliendelea kuulizwa huku Mustapha akipakiwa ndani ya gari ili apelekwe hospitali,jeraha alilopigwa risasi lilivuja damu nyingi.
“Na nan a na naitw..a So..nia Sooonia Shayo”
“Sonia nani?”
“Sha…yo”
“Ilikuwaje?”
“Nil..kuwa nyumba..ni kwang..u mid..a ya saa mbi..li nikas..ikia mlan…go….”
Sonia alijielezea kila kitu,hakuacha chochote kile.Bado aliendelea kulia machozi ya kwikwi huku akiwashukuru watu waliokuja kuyaokoa maisha yake ndani ya msitu wa madale.
“Sisi ni wanajeshi,yule aliyepigwa risasi ni mwenzetu.Tushapiga simu polisi wanakuja sasa hivi”
“Ahs..ante sana”
“Unaishi wapi?”
“Mikocheni B”
“Ngoja tukupeleke il…”
“Hapana kaka,msinipeleke ninaogopa nitalala hotelini tu”
“Kweli?”
“Ndio”
Hivyo ndivyo ilivyokuwa,Sonia alipakiwa ndani ya gari na wanajeshi kumsindikiza mpaka Tegeta mwisho hapo walimtafutia Sonia hotel.
“Sasa nyie mnaweza mkaenda,mimi niacheni na huyu binti niendelee kumuhoji maswali”
Mmoja wa wanajeshi aliyefahamika kwa jina la Shadrack Libaba alitoa pendekezo.
“Sawa,sisi wacha turudi Madale,alafu Nasra kanipigia simu Mustapha yupo Aghakhan,inabidi tuhakikishe hili swala linafika mahali husika”
“Hakuna shaka”
“Basi sawa,usiku mwema”
“Ok!”
Ulikuwa ni usiku tayari,Shadrack na Sonia wakaongozana mpaka chumbani.Kwa msaada aliopatiwa Sonia hakuelewa ni aina gani ya shukrani aitoe, kwake ulikuwa ni zaidi ya msaada licha ya kufika hotelini bado alionesha kuwa na wasiwasi, bado hakuamini kama amepona na wakati mwingine aliona mambo yaliyotokea yalikuwa ni kama ndoto,picha ya kufungwa kwenye mti na kutakwa kupigwa risasi bado viliendelea kupita kichwani mwake,akabaki amekaa kitandani analia machozi.
“Sonia”
Shadrack aliyekuwa juu ya kochi aliita.
“Abee”
“Usijali,kila kitu kipo sawa”
“Ahsante”
Sonia akaingia bafuni kujimwagia maji na kurudi chumbani akiwa amejifunika na shuka mwili mzima.
“Sasa utalala wapi kaka?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Sonia.
“Mimi silali,si unajuwa sisi wanajeshi”
“Kitanda hiki kikubwa njoo ulale tu”
“Usijali wewe lala tu”
Shadrack alitoa msaada na alikuwa yupo radhi kuhakikisha kuwa Sonia anakuwa salama kabisa mpaka kunakucha,alijitolea kutoa msaada huo kwa moyo mkunjufu! Ni kweli mpaka kunakucha siku hiyo alikuwa macho.
Kitu cha kwanza Sonia baada ya kuzinduka kutoka usingizini alijikagua,hakuwa na Imani na mwanaume yoyote yule,alikuwa na uhakika kuwa hajaingiliwa kimwili lakini ilimbi-di ahakikishe swala hilo kwanza.
“Za asubuhi”
Shadrack ndiye aliyetoa salamu.
“Nzuri”
“Naona umeamka,nikuletee chai?”
“Hapana usijali kaka angu,nitaenda tu mwenyewe”
“Sawa”
Tangu siku hiyo,Sonia na Shadrack walikuwa marafiki wakubwa sana.Sonia hakutaka kurudi nyumbani na swala hilo Shadrack akaliunga mkono,aliamini bado anatafutwa auliwe na watu ambao hakujua wametumwa na mtu gani.Sonia alishangazwa na kitu kimoja tu kutoka kwa Shadrack,macho yake.Hakumuangalia kwa macho ya kawaida,kuna kitu alijifunza kupitia macho ya mwanamue huyo.Alimuomba Mungu yasiwe mambo anayofikiria,aliogopa kumuuwa mtu asiyekuwa na hatia,Shadrack hakustaili kufa.Msaada aliompa ulikuwa mkubwa sana!
“Shadrack”
Sonia aliita siku hiyo usiku wakiwa chumbani,Shadrack akiwa juu ya sofa.
“Naam Sonia”
“Una mke?”
“Hapana”
“Mh!”
“Mbona umeguna?”
“Okay,una mwanamke?”
“Sina”
“Kwanini?”
“Kwa sasa hivi bado nina mawazo”
“Kwanini sasa?”
“Mke wangu alifariki”
“Oh! Maskini pole sana”
“Nishapoa”
“Aliumwa?”
“Hapana,alipata ajali ya gari”
“Pole sana”
“Nishapoa”
Kama ungemuangalia Shedrack usoni usingegundua kuwa anadanganya,ukweli ni kuwa alikuwa ana mke amemtelekeza Mkoani Sumbawanga na watoto watano,katika akili yake alikuwa na mahesabu makubwa juu ya Sonia,hakuwa hapo kutoa msaada wa bure.Sonia alihitajika kingono ndiyo maana alikuwa akimuangalia kwa macho ya matamanio.
“Aya Usiku mwema”
Shadrack hakuitikia,bado alikuwa akifikiria ni njia gani atumie kumuingia Sonia.Akili yake ilimtuma atumie nguvu lakini aliogopa ingekuwaje endapo mwanamke huyo atamshtaki,aliogopa kufungwa jela.
“Kwani kitu gani?nitatumia nguvu tu.Si nina bastola,akikataa nitamtishia kumuuwa”
Hayo yote aliwaza Shadrack huku akimuangalia Sonia aliyekuwa kitandani,anageukia upande wa pili.Sio siri uzuri wa mwanamke huyo ulimchanganya akili yake,angejiona boya au fala endapo angeshindwa kumfanya chochote siku hiyo, hapohapo sehemu yake ya uzazi taratibu ikaanza kusimama!


****
Sebastian alilala kitandani kwa takribani siku nne bila kujua chochote kinachoendelea Duniani,Wauguzi kila siku waligongana ndani ya wodi lake V.I.P, ambapo kila kitu kilikuwepo ndani.Madaktari wa kihindi walijitahidi kadri wanavyoweza ili kuyaokoa maisha ya mtoto huyu wa tajiri, Waytte.Tayari walishakula pesa za kutosha ambazo zilikuwa nyingi kuliko hata mishahara yao,ndiyo maana walishughulika naye na kila wakati walikuwa pembeni yake,usiku wa saa mbili siku ya tano Sebastian aliyafumbua macho yake akiwa kitandani,mtu wa kwanza kumuona alikuwa ni mama yake mzazi.
“Seb..astian”
Mama akaita na kumsogelea mwanaye kipenzi,kwake ulikua ni kama muujiza kutokana na hali aliyofikia Sebastian ya kutoa mapovu mdomoni, ilimfanya aamini kuwa angemkosa na hakuelewa angezipokea vipi habari za mwanaye kufa,alikuwa ni mtoto wake wa pekee.
“Moo..m”
Sebastian akajikaza na kuita,kumbukumbu zake taratibu zikaanza kujikusanya.Alikumbuka kila kitu kilichotokea mpaka akafikishwa mahali hapo.Picha ya Sonia ilivyomjia alijikuta anabana meno yake kwa hasira,hakuelewa ni kwanini anamchukia mwanamke huyo.
“Doktaaaa…Doktaaaa”
Mama akamuita Daktari wote wakaingia haraka,hata wao walishangazwa na maendeleo ya Sebastian maana hawakuwa na matumaini kuwa atazinduka siku kama hiyo.

Hali ya Sebastian kuanzia siku hiyo ikawa inaendelea vizuri,siku iliyofuata aliruhusiwa kutoka hospitali na kuandikiwa dawa chache za kumeza.
Mr.Waytte bado hakuelewa ni kitu gani kiliendelea,askari aliowatuma wamuuwe Sonia alipoteza mawasiliano nao,hakuwapata hewani, kitu hicho kilimtia hofu sana,hakuelewa ni kitu gani kiliwapata.Alielewa ni kituo gani cha kuwapata lakini alihofia kukamatwa endapo mpango wake ungekuwa wazi na upande mwingine wa akili yake ulimtuma kuwa polisi aliowatuma wamekamatwa na hapo alipo anatafutwa.
Hakuelewa ni kitu gani akifanye.
“Hawa washenzi nao mbona hawapatikani?au washakamatwa”
Hilo ndilo swali alilojiuliza Mr.waytte kila siku iendayo kwa Mungu wake.Jambo lingine lililomuuma zaidi ni habari za mwanaye kuambukizwa ugonjwa wa Ukimwi,japokuwa hakutaka kulipa jambo hilo kipaumbele!
“Lazima nijue ukweli”
Ulikuwa ni usiku wa saa mbili, Mzee Waytte akatoka chumbani kwake na kwenda kumgongea mwanaye mlango.
“Mimi baba yako”
Mzee Waytte akajitambulisha baada ya Sebastian kutaka kujua nani anayegonga mlango wake.
“Nakuja”
Mlango ukafunguliwa,Sebastian akawa anafikicha macho ilionekana alikuwa ameshtuka kutoka usingizini.
“Vipi ulikuwa umelala?”
“Ndio,naona dawa zinaniendesha kidogo”
“Pole sana,daktari amenipigia simu twende hospitali”
“Kuna nini tena wakati teyari tushamalizana”
“Hata mimi sijui”
Mr.Waytte hakutaka kumuweka mwanaye wazi kwa kitu anachotaka kukifanya,ilikuwa ni lazima ajue afya ya mwanaye kama ni kweli ana virusi vya ukimwi alitaka airidhishe nafsi yake.Hakuwa na jinsi zaidi ya kumsikiliza baba yake wala hakuwa anaelewa anaenda kupimishwa damu kubwa,dakika kumi zilimtosha akawa tayari amevaa nguo zake.Wakatoka na baba yake mpaka nje kwenye maegesho ya magari,wakaingia.



*******
ENDELEA KUSOMA HADITHI NA SIMULIZI ZA MTUNZI….EMMANUEL F.KWAY(THE STORY MASTER)

0 comments:

Post a Comment

BLOG