Search This Blog

Sunday, May 31, 2020

SLAVE SEX SEHEMU YA 4/10


SLAVE SEX
MTUNZI….EMMANUEL F.KWAY(THE STORY MASTER)
AGE…(18+)
WatsApp…+255718 862176
SEHEMU YA 4 KATI YA 10
*******


“Nani Sonia?”
“Ndio Dad ni mimi?”
“Enhee niambie mwanangu, vipi masomo?”
“Baba nimefukuzwa shule”

“Umefukuzwa shuleeee?”
“Ndio Baba”
“Kwanini?”
“Baba nitakwambia ila naomba usikasirike tafadhali”
“Sasa umefukuzwa shule mbona sijaambiwa?”
“Dad utapigiwa sasa hivi”
“Okay mwanangu,njoo nyumbani”
Ni kweli baada ya kushusha pumzi na kukata simu na kabla ya kuzungumza kitu chochote simu yake ikaita tena, hii aliigundua ilitokea nchini Uganda sababu ilianza na ‘code’ +256, akavuta pumzi na kuelewa nini kinaendelea.
Ni kweli kama alivyowaza kwani simu hiyo ilitoka kwa mkuu wa shule Mr.Edward Kiwanuka,akimwambia kwamba Sonia amefukuzwa shule moja kwa moja.Nickson akajaribu kila jitihada ili kumtetea binti yake aendelee na masomo lakini ikashindikana ikabidi tu akubali.
Maongezi hayo yalivyokuwa yanaendelea Pendo na Mariam walikuwa kimnya wanafatilia kila nukta ya mazungumzo anayofanya Nickson akionesha kuchanganyikiwa.
“Okay fine, it’s okay for me, let’s do this Mr.Kiwanuka, I’ll send air ticket to your email today.Thank you”
Jitihada za kumshawishi mwalimu huyo ziligonga mwamba, Nickson akawa anaongea kwa hasira,akitaka kumtumia mwalimu huyo tiketi ya ndege haraka iwezekanavyo siku hiyo ili Sonia mtoto wake anayempenda arudi nyumbani.Hapo hapo baada ya kukata simu aliingia chumbani kwake akiwaacha Pendo na Mariam wakimshangaaa lakini Pendo hakutaka kubaki juu ya sofa,akasimama na kumfuata Mpenzi wake chumbani.
“Baba, Vipi tena?”
Pendo aliuliza.
“Sonia kafukuzwa shule naenda kumkatia Tiketi mara moja hapo Posta arudi kesho asubuhi”
Nickson alijibu haraka haraka huku akibonyeza bonyeza simu yake, akaiweka mfukoni na kubeba funguo za gari.
“Si uwende baadaye”
“No,wacha niende sasa hivi”
Pendo hakuwa na uwezo wa kumzuia Nickson tena,akamuacha aondoke zake.Akatoka mpaka nje na kuingia ndani ya gari akaanza safari ya kuelekea Posta,dakika arobaini na tano baadaye akawa amefika.
Hapo aliingia na kumtafuta mkurugenzi Deo Karekezi.
“Mr.Shayo karibu kiti,niambie wapi tena unataka kusafiri?”
Kijana huyo alimchangamkia Nickson,kutokana na kuwa mteja wao walijikuta wamejenga urafiki.
“Nahitaji Tiketi ya Rwandair,embu nikatie ya kesho saa nane mchana kama ipo”
“Okay sawa”
Kijana akatupa macho yake juu ya kioo cha Kompyuta,akabonyeza bonyeza keyboard.Baada ya hapo akaibua shingo yake na kumtizama Nickson.
“Ipo hapa tayari nafasi zipo,nimepata unaweza ukalipia”
Nickson akafurahi,alichofanya ni kutoka nje na kununua dolla za kimarekani ili kulipia tiketi,taratibu zilivyokamilika akachukua tiketi na kumuomba bwana Deo Karekezi amsaidie kuituma tiketi kwa njia ya Email ili imfikie mkuu wa shule,Mukono Parent’s high school.JAMBO HILO LIKAWA LIMEKAMILIKA ndani ya dakika tano.
“Ahsante sana”
Nickson akaaga na kuondoka zake,akiwa na mawazo chungu mzima!
***
Ndege ya shirika la Rwandair liliweka matairi yake juu ya uwanja wa mwalimu Nyerere Saa kumi ya jioni,ikatingishika kidogo na kukaa sawa hapo ilichomoka kwa kasi ya mshale kisha ikaanza kutembea taratibu mpaka ikasimama kabisa,kwa mujibu wa ratiba zilivyopangwa hiyo ndiyo ilikuwa ndege aliyokuwa akiisubiri Nickson Shayo tangu saa saba ya mchana,alikuwa akimsubiri Sonia kwa usongo na muda wote sura yake ilionesha kutabasamu.

Akiwa katika viti vya watu wanaosubiri wageni akasikia sauti nyororo kutoka katika vipaza sauti kwamba Rwandair tayari imeshatua.Akasimama mpaka karibu na mlango wa kutoka wageni.Baada ya dakika kama sita hivi watu wakaanza kutoka mmoja baada ya mwingine.
Macho ya Nickson hakuyachezesha hata kidogo muda wote alikuwa makini akiwatizama watu wanaotoka.Ghafla akaanza kuhisi baridi la ghafla,abiria walikuwa wameisha ndani ya ndege akachungulia ndani kabisa,hakukuwa na dalili yoyote ile ya Sonia kutokeza.
“Excuse me,Excuse me”
Nickson akaita,baada ya kuwaona wahudumu wa ndege wakiwa katika sare huku mbele wakiongozwa na ma ‘pilot’ wakiwa katika sare zao maalumu wanaburuza mabegi.Mmoja wa wahudumu akasimama.
“Samahani,pole na kazi”
“Ahsante”
“Wewe ni mfanyakazi wa shirika la Rwandair?”
“Ndio”
“Kuna binti yangu simuoni na alipanda humu”
“Oh,sasa embu nenda pale mapokezi ukaulize”
“Ahsante”
Nickson akageuka akatembea hatua tano tano mpaka kwenye sehemu aliyoelekezwa,akajitambulisha na kueleza shida yake.
“Subiri kaka angu kidogo”
Mrembo aliyekuwa mapokezi alijibu na kuchukua mkonga wa simu.Akajielezea kwenye simu.
“Binti yako anaitwa nani?”
Binti wa mapokezi akamuuliza Nickson huku akiwa amefunika mkonga wa simu kwenye maiki,ilielekea simu hiyo ilikuwa hewani na ilisubiri jibu la Nickson Shayo.
“Anaitwa Sonia Nickson Shayo”
“Okay”
Msichana wa mapokezi alivyorudi kwenye laini akataja jina,akasubiri kwa kama sekunde tano.
“Kaka samahani,inavyoonesha kuwa binti yako hakupanda hiyo ndege lakini tiketi ilikatwa”
Nickson alimtizama msichana huyo bila kummaliza,akahisi uti wake wa mgongo unapigwa na baridi.


****

Shule ilikuwa kimnya na ilijaa simanzi kupita kiasi,wanafunzi wote walikuwa wamekusanyika asubuhi mstarini wakisubiri matangazo lakini siku hiyo ilikuwa tofauti.
Mbele walisimamishwa wanafunzi wa kike wawili wakiwa wanalia machozi.Ni dhahiri kuwa walionesha hali isiyo ya kawaida,baadhi ya wanafunzi walikuwa tayari wanaelewa nini kitakacho tokea.Baada ya matangazo na adhabu tofauti kutolewa mbele ya jopo la wanafunzi,mkuu wa shule Mr.Edward Kiwanuka akatokea akiwa ameukunja uso wake.Akapita mpaka mbele kabisa akawasalimia wanafunzi wote.
“You are here to study not otherwise!You know It hurts when you chase someone’s daughter or son, i am also a parent.I understand that situation when it comes as a parent its so painful.Pull yourself together.Put yourselves under my shoes as a parent and feel it.Today am going to suspend this fools Zawadi and Sonia Shango,Shayu whatever I don’t care.You Sonia, do you know how much your Dad plead to me because of you? he was almost crying”(Mpo hapa kwa ajili ya kusoma si vinginevyo.Inauma kumfukuza mtoto wa mtu shule mimi pia ni mzazi naelewa likija swala hilo,inauma sana kama mzazi.Embu zingatieni,jifanye wewe ndiye mimi kama mzazi.Leo naenda kuwasimamisha shule hawa wapumbavu Zawadi na Sonia.Wewe Sonia,unajua ni kiasi gani baba yako amenisihi kwa ajili yako,alikuwa akitaka kulia)
Mr.Edward alizidi kuzungumza huku akiwatizama wanafunzi wake,ilikuwa ni siku ya huzuni kwa waliowafahamu wanafunzi hao wawili hasa kwa watanzania wenzao.
Machozi yalikuwa yakiwalenga.Mr.Edward Kiwanuka akazidi kuongea.
“Do you know how many borders you cross from Tanzania to Uganda?okay lay down go down, I have to cane you”
Mr.Edward alipandwa na hasira akakasirika kupita kiasi, nyuma ya adhabu hiyo alikuwa ana kisasi cha kukataliwa na Sonia,alivyomtizama mwanafunzi wake alivyokuwa mzuri ndiyo akapandisha mori alitaka kumkomoa,akamsogelea na kumvuta kwa nguvu huku akimshika shingo akitaka kumlaza chini kilazima.
“Lay down stupid”(Lala chini mjinga)
Alizidi kuongea kwa hasira na kushika bakora kubwa iliyofananishwa na gongo,alivyoiweka mkononi vizuri akaishusha mgongoni mwa Sonia,kila mwanafunzi alishtuka jinsi gongo hilo lilivyotua,Sonia akaachia ukulele wa maumivu.

Partson Ngogo aliyekuwa nyuma kabisa alishuhudia kila kitu akatamani kusogea mbele na kama lolote alianzishe sababu aliamini kwamba kufukuzwa kwa Sonia shuleni hapo hakukuwa na maana yoyote ya yeye kuendelea kuwepo na kama mbwai iwe mbwai!
“Oyaa P,ticha anazingua ujue yule mtanzania mwenzetu,atampiga vipi wakati keshamfukuza shule kama vipi tulianzishe”
Sauti nzito ya Mwanafunzi aliyeitwa Bright Kimaro ikasikika nyuma ya Partson.
Maneno hayo yakamtia nguvu,akajikuta anachomoka mstarini mpaka mbele kabisa akamshika Mr.Edward Kiwanuka mkono uliokuwa unazidi kumpiga msichana aliyempenda kuliko kitu chochote kile chini ya jua la Mungu na huo ndiyo ulikuwa wakati wake wa kuonesha penzi la Kweli, ilikuwa ni bora afukuzwe shule kuliko kuendelea kushuhudia jambo hilo la kinyama linatokea.
MAMBO tayari yalishaanza kuharibika tayari, Sonia alisimama na kutokuamini kitu kilichotokea.
“Huwezi kumchapa nasema,si ulishamfukuza shule?”
Partson akasema akiwa bado kamshika Mwalimu Mkuu mikono.
“Una mtetea Malaya wako sio?”
“Ndio nakwambia ukweli”
“Partson,usinitafutie balaa nafukuza shule nawewe”
“Poa”
Ghafla ikawa vuta n’kuvute wanafunzi wakaanza kusogea mbele, hali ya hewa ikachafuka.
Kwa kitendo kilichotokea ilibidi Partson aitwe ofisini akiwa pamoja na Zawadi na Sonia.Barua tatu zikachapwa hapo hapo wakapewa,wakawa wamefukuzwa shule lakini kabla ya Partson kufika getini Mwanamke mnene akatokeza,akashuka ndani ya gari, huyu alikuwa ni Mmiliki wa shule yaani ‘Director’.
“Njoo Partson”
Partson akatembea mpaka karibu na gari,akasalimia.
“Nini tatizo?”
“Mr.Kiwanuka kanifukuza shule”
“Kwanini?”
Partson akaanza kujieleza kila kitu kinagaubaga mpaka mambo yalivyotokea.
“Njoo ofisini”
Mama mwenye shule pamoja na Partson wakaongozana mpaka Ofisini na Mr.kiwanuka akaitwa akakaa juu ya kiti.
“Huyu mwanafunzi abaki hapa,unaelewa kabisa ndiyo tunamtegemea shule nzima sasa inakuwaje unachukua maamuzi hayo?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Mama mwenye shule.
“Anastaili kufukuzwa shule,sasa kwahiyo aendelee kufanya fujo kisa yeye ndiye tunamtegemea?”
“Unajua shule ngapi wanamuhitaji huyu mwanafunzi?unajua ni kiasi gani kaipa shule yetu pesa?basi mimi nasema kwamba huyu afukuzwi,Partson nenda darasani”
Ilikuwa ni kauli ambayo hakuna hata mmoja angeweza kuipinga.Bosi keshatoa kauli, Edward Kiwanuka angekataa?asingeweza.Akajizoa zoa kwa aibu na kutoka ofisini.
“Partson nenda darasani ukajisomee”
“Ahsante Mama”
“Sawa”
Ilikuwa ni furaha kubwa sana kwake ukweli ndiyo ulikuwa huo,kumfukuza Partson Ngogo shule kulimaanisha shule hiyo kuyumba, kwani alikuwa ni tegemezi kubwa kwake,kipaji chake cha kucheza mpira kikawa kimemuokoa.Haraka akatembea mpaka getini.
“Sonia”
Partson akaita kabla ya Sonia kutoka getini na mabegi yake, akageuka huku machozi yakiwa yanamlenga.
“Ahsante Partson,sijui nikushukuru vipi,sina jinsi nyingine Zaidi ya kusema ahsante”
“Sisi sote ni watanzania,lakini jua kitu kimoja ningetamani siku moja tuwe wapenzi nakupenda sana itaniuma sana kutenganishwa nawewe,japokuwa ulikuwa hutaki kuongea namimi kila nikitaka iwe ivyo,nakupendsa Sonia nakupenda sana”
Partson Ngogo aliongea kwa hisia zote akatumbua jipu lililokuwa ndani ya mtima wake siku zote tangu amuone msichana huyu mzuri.
“Ahsante Partson,kila la kheri”
Hilo ndilo jibu alilojibu Sonia,Partson akabaki njiapanda hakujua lina maana gani, akabaki akimuangalia anavyotoka getini huku akiburuza mabegi akatoka mpaka nje ya geti akiwa analengwa na machozi, akahisi moyo wake una kitu haujatendewa haki.
Akageuka nyuma akamtizama Partson, macho yao yakagongana wakawa kama wanaongea kwa macho.Aliyekuja kuwatoa kwenye mawazo hayo ni Zawadi Kasanga akitoka nje, wakaungana na Sonia tayari kwa safari ya kwenda majumbani kwao.
“Sonia”
Zawadi akaita.
“Abee”
“Hii ni tiketi yako nimepewa na Kiwanuka”
“Ahsante”
Hao wakaanza kujikongoja taratibu mpaka walipofika stendi ya magari iliyoitwa Kigunga, wakapanda daladala mpaka Kampala.
“Mimi Sonia nitaondoka Keshokutwa nadhani, wewe tiketi yako inasema Kesho,kwahiyo nakutakia safari njema ipo siku tutaonana tena”
“Usiseme ivyo,kwani huu sio mwisho wetu”
“Mimi ndiye niliyesababisha lakini”Hivyo ndivyo ilivyokuwa, wakatafuta Hotel wakalala, mpaka kesho yake Sonia akanyoosha mpaka uwanja wa ndege Entebbe akiwa na majonzi mengi kupita kiasi,kichwani mwake alimuwaza Partson moyo ulimuuma kwa kiasi cha kutosha, akatamani arudi shuleni lakini akahofia ndege kumuacha,akabaki kuitizima Tiketi iliyokuwa mkononi mwake,ikiwa ni masaa machache ndege hiyo ianze safari.Akazidi kuwaza na kuwazua, akashuka ndani ya daladala baada ya kufika chuo kikuu cha Nkumba,akasimama na kutembea mpaka zilipo taxi.
“Entebbe Airport, how much?”(Kiwanja cha ndege cha Entebe ni kiasi gani)
Sonia akauliza baada ya kukaa siti za nyuma,ndani ya taxi.
“Mutwalo,njagala mutwalo”(Elfu kumi,nipatie elfu kumi)
Dereva taxi akajibu kilugha cha kwao kabla ya kuwasha gari.
“It’s okay”
Kauli hiyo ilivyotoka, gari ikawashwa na safari ikaanza hapohapo.
Baada ya dakika kumi walikuwa katika lango la uwanja wa ndege entebe, dereva akapewa kadi akazidi kusonga mbele,wakaenda mpaka kwenye maegesho ya magari.
Sonia kabla ya kushuka akatoa noti ya shilingi elfu hamsini ya kiganda,akasubiri chenji yake.
“Sasa mbona hukuniambia kama una pesa kubwa?hayo ni makusudi dharau izo”
“Samahani,sikujua kaka angu”
“Mnazingua bwana”
Dereva taxi akakasirishwa akatoka ndani ya gari akiomba Chenji,dakika kumi na tano nzima zikapotea kutokana na kutafuta chenji, kwa jinsi mawazo aliyokuwa nayo Sonia hakuelewa ni kiasi gani muda unakwenda na alitakiwa awahi ndege.
“Kamata hiyo”
Dereva akatoa shilingi elfu arobaini na kumkabidhi mteja wake huku akiendelea kubaki na gubu kama ndugu wa mume!
“Mademu wengine sijui vipi”
Dereva akajisemesha huku akiondosha gari.
Sonia wala hakuangaika naye akatembea taratibu mpaka mapokezi.Akachanganyikiwa alivyoambiwa kuwa amebakiza dakika tano tu za kuwepo mahali hapo na kwamba abiria wote wanaosafiri wapo ndani ya ndege.
“Embu wahi,jaribu bahati yako”
“Sawa dada”
Sonia akaanza kutembea kwa haraka huku akiburuza begi lake, akaingia kwenye ukaguzi lakini alikuwa keshachelewa tayari kwani geti lilikuwa limefungwa kumaanisha kwamba hakukuwa na namna yoyote ile ya kuweza kupita getini.Akasikitika sana akarudi na kuendelea kukaa juu ya benchi akashindwa kuelewa ni kitu gani akifanye.
****
Nickson aliendelea kupata wasiwasi usio wa kawaida,kitendo cha kutopata jibu la wapi Sonia alipo kilimchanganya akili yake,akili yake ikashindwa kufanya kazi sawasawa, njia pekee aliyotumia ni kupiga simu moja kwa moja kwa Mkuu wa shule Uganda,jibu alilopewa likazidi kumchanganya akili yake.Aliambiwa kuwa Sonia alishaondoka na sio mwanafunzi wa hapo tena alishafukuzwa.
Wazo lingine likamjia akampigia mkurugenzi Deo Karekezi aliyemkatia tiketi ya ndege,alimuelezea kila kitu kwa kifupi.
“Kwamba mwanao hayupo ndani ya ndege?”
“Ndio,hayupo namimi nipo hapa Mwalimu Nyerere,inakuwaje?”
“Subiri usikate simu”
Simu ikabaki hewani, ikasikika Deo anaongea na mtu mwingine kwenye simu tena kwa lugha ya kiingereza akajua ni wazi kuwa simu alipiga Uganda kwenye shirika la ndege,akasikia neno ‘thank you once again’akajitayarisha kupokea habari za upande wa pili.
“Nickson”
Deo akarudi kwenye laini.
“Ndio Deo,nakusikiliza”
“Mwanao alionekana uwanja wa ndege kweli,wameniambia kuwa watatumia CCTV camera kumsaka kama bado yupo uwanjani,embu usikate simu napigiwa hapa nadhani ndiyo hao….”
Deo akapokea tena simu kutoka Uganda,safari hii aliongea huku akitabasamu akarudi tena kwa Nickson.
“Wamempata,sasa hivi yupo mikononi mwa Walinzi,yuko salama”
“Tafadhali naomba nizungumze naye ili unitoe wasiwasi”
Haikuchukua hata dakika tano akawa hewani na Sonia.
“Sonia mwanangu mzima?”
“Baba mimi mzima,samahani nilichelewa ndege tu, lakini kila kitu kipo sawa kabisa”
“Sasa nataka nikukatie ndege nyingine ya Usiku,subiri hapohapo sawa mwanangu”
“Okay Dad”
Simu ilivyokatwa Nickson akamtafuta Deo Karekezi kwa mazungumzo ya utaratibu wa kukata tiketi siku hiyo,kweli ilipatikana AIR UGANDA ya usiku wa saa tano.
Mambo yakaenda haraka, tiketi ikatumwa Sonia akawa anasubiriwa.Saa sita kasoro ndege ya Shirika la ndege ya AIR UGANDA ikawa imehitimisha safari yake Tanzania,Dar es salaam uwanja wa kimataifa mwalimu Nyerere.Haikuchukua muda sana Nickson akamuona Sonia anaburuza begi lake.
“Soniaaa”
Nickson akaita,Sonia akamsogelea baba yake na kuanza kutoa machozi ya kujuta kwa kile alichokifanya.
“Da..d nisame..he najua nimekukosea”
“Usijali usijali,usijali usilie twende kwenye gari pole na safari”
“Ahsante baba”
Nickson akashika begi la mwanaye wakanyoosha mpaka kwenye maegesho ya magari.
Wakaanza safari ya kurudi nyumbani.

Kwa kuwa hakukuwa na msongamano wa magari na ukimnya haikuwachukuwa muda mrefu wakawa wamefika Sinza kwa Remmy.Wakakunja kushoto wakanyoosha, hapo gari likaingia kulia na kuiacha barabara ya vumbi,dakika moja tu wakawa wamefika nje ya geti kubwa jeusi.
Geti likafunguliwa na mlinzi.Moyo wa Sonia ukawa umechanua ukapiga mkambo,akatabasamu alifurahi sana kufika nyumbani ni miaka mingi sana ilipita.Akashuka na kupita ndani lakini jambo moja lilimchanganya akili yake, ni baada ya kumuona Mwanamke akiwa na mtoto mdogo akitokea chumbani mwa baba yake,kwa akili ya ki utu uzima aliyokuwa nayo alishaelewa nini maana yake, ingawa alikuwa na jibu kichwani lakini hakutaka kulipa nafasi ya moja kwa moja.
Kabla ya kusalimia akamgeukia Baba yake ambaye alikuwa anamalizia kufunga mlango.
“Mama yuko wapi?”
Sonia akatupa swali kwa Baba yake.
“Mama yako hayupo,huyo unayemuona ndiyo atakuwa mama yako kwahiyo nachok…..”
“Daaaaad….”
Sonia hakutaka tena kuongea kitu kingine, alichofanya ni kupita moja kwa moja chumbani kwake akaingia na kubamiza mlango kwa nguvu,akiashiria kukasirishwa na kitendo hicho.

 Hakukuwa na namna yoyote ya kumshawishi Sonia akubaliane na hali iliyotokea kwamba mama yake amefukuzwa na yupo mama mwingine,ni jambo ambalo hakutaka kukubaliana nalo habadani!
“Sonia”
Nickson akamuita mwanaye kwa unyonge baada ya kuingia chumbani kwake lakini hakuitikiwa,Sonia hakujibu lolote japokuwa alisikia akiitwa.
“Sonia,amka nikwambie kitu,tafadhali mwanangu”
“Nakusikiliza Baba,ongea”
Sonia akasema bila ya kuinua shingo yake.Kichwa chake kikawa kimezama ndani ya mikono yake.
“Wewe bado mdogo sana kujua ni kitu gani kilichotokea, lakini nachokuomba mwanangu usijisikie vibaya,huyu unayemuona hapo ni mama yako pia vile vile anakupenda sana”
Nickson akazidi kumsihisi mwanaye,nusu saa lizima akawa anamuimbisha na kumwambia kila kitu kilivyokwenda lakini hakuthubutu kumueleza ni kitu gani kilitokea mpaka akamfukuza Mama yake.
“Na yule mtoto unaye muona ni mdogo wako anaitwa Brenda”
Nickson akazidi kuongea, hakuwa na sababu ya kuficha kwa sababu ukweli ulijionesha wazi.Hakukuwa na sababu ya kuukata ukweli, ilibidi Sonia akubali kishingo upande jambo hilo akaliweka kando,ili maisha yaende.

****
Pendo Jonas au Mama Brenda mbali na Sonia kutokuwa mwanaye wa kumzaa lakini alimpenda kupita kiasi, akampa mapenzi yote ambayo Mama anatakiwa kumpa mwanaye huku akizidi kumuhimiza Nickson juu ya swala la shule,jinsi mambo yalivyokuwa yanaenda Sonia akajikuta anakubaliana na hali,akampenda pia Pendo.Akamchukulia kama ni mama yake wa kumzaa.
“Soniaaa”
“Abee Mama”
“Chai tayari mwanangu”
“Sawa Mama namalizia kuvaa”
Baada ya dakika moja Sonia akawa mezani na Mama yake wa kufukia lakini yeye akamchukulia kama mama yake mzazi, akambeba mdogo wake Brenda akaanza kucheza naye.
Hapo hapo akatokeza Nickson wakaungana mezani wakaanza kunywa chai nzito ya maziwa ikiambatana na vitafunio vya kishua kama Kuku,soseji mkate wenye siagi na mazaga yote,meza ikawa imechafuka, kila mtu aligusa kitu anachokitaka.
“Sonia shule vipi sasa?Upo tayari lini kuanza?”
Nickson akauliza huku akiwa na kipande cha mkate uliopakwa ‘Blueband’ ya kutosha.
“Mimi hata kesho Dad”
“Nimekutafutia shule Australia”
“Daaad,mimi sitaki kukaa mbali na nyumbani”
Sonia hakupendezwa na kauli ya baba yake, mbali na hapo hakutaka tena kukaa mbali na familia yake,alimpenda sana baba yake.
“Sonia,hapana mimi nina maana yangu kukwambia ivyo kukaa nje ya Tanzania itakujenga sio kwamba sikupendi hapana,lakini ukikua utajua nini maana yangu hapa sasa hivi huwezi kujua,bado mdogo”
“Lakini baba Sonia”
Pendo akaingilia mazungumzo, wote wakamgeukia.
“Naam”
“Kwanini usimsikilize mtoto?yeye amekwambia hataki wewe msikilize ni wapi anataka kwenda kusoma”
“Hapana,siwezi kumuacha Sonia asome hapa”
“Mimi sitokubaliana na wewe hata kidogo,hiyo inakuwa sio haki,mpe haki mtoto”
Mara ukazuka mvutano Nickson akajikuta kasimama mwenyewe upande wake,kutokana na mambo yalivyotokea hakuweza kubisha ilibidi akubali hali halisi,Sonia alifurahi sana.
Kuanzia siku hiyo nyumba ilijaa furaha mno,Sonia na Pendo walipendana utadhani mtu na mama yake ukweli, pia alimhangaikia kumtafutia shule wakishirikiana na Nickson.
Sonia alitakiwa kuanzishwa kidato cha tano haraka iwezekanavyo,hatimaye walipata shule nzuri,ikabaki tu wafanye malipo kisha Sonia aanze masomo,hilo halikuwa na shida yoyote siku hiyo ya Jumamosi Nickson akaenda CRDB bank mlimani City, akafanya malipo kisha kurejea nyumbani na risiti ya Benki.
“Sonia,Jumatatu utaenda shule,nishalipa kila kitu”
Nickson alishakamilisha malipo na kumkabidhi Sonia kila alichotakiwa kupewa kama mwanafunzi.Kwa furaha waliyokuwa nayo siku hiyo mchana walipanga kutoka kwenda kutembea sehemu mbali mbali za jiji.
Wote wakajiandaa wakaingia ndani ya gari wakiwa wenye furaha kupita kiasi,ilikuwa ni familia yenye furaha na iliyopaswa kuigwa.
***
“Naomba msaada,naomba msaada”
Sauti ya mwanamke mchafu aliyevaa nguo zilizochanika alikuwa katikakati ya msongamano wa magari akipita kila sehemu kuomba chochote kitu,kutokana na uchafu wake na mwili wake kupungua uzito hakutofautishwa na chokoraa wa mitaani au teja.
Ungebahatika kupewa picha yake na ungeambiwa kwamba ndiye huyu Gloria aliyekuwa akitesa miaka iliyopita wallah usingekubali.
Gloria alikonda na kupungua uzito mara tano yake,usoni alijawa na vipele vingi huku mdomoni kukiwa kuna utando mweupe kama kinda la njiwa, muda wote alikuwa akikohoa mfululizo.Historia yake ya nyuma kila akiikumbuka alikuwa akilia machozi,alijuta kupita kiasi,akatamani mambo yanayotokea ayapindue yawe katika mstari lakini haikuwa ivyo,ukweli ulibaki kwamba ni muathirika wa ugonjwa hatari wa Ukimwi tena anayesubiri kufa muda mchache ujao,kazi yake ilikuwa ni kutembea barabarani na kuomba misaada.Kuona thumni ya shilingi mia kwake ilikuwa ni bahati kubwa.
“Naomba msaada,nisaidie si..jala”
Gloria alisema baada ya kioo cha gari kufunguliwa Mama mtu mzima akatoa noti ya shilingi mia tano na kumkabidhi,hakuamini macho yake, moyo wake ukapiga mkambo.
Haraka akatembea mpaka kwenye kibanda cha mama N’tilie na kuagiza chakula,siku hiyo alijiona bilionea, akala na kunywa maji,akashiba.

Usiku ulivyoingia akatafuta kiboxi chake ambacho alikifanya ni godoro, akaweka kibarazani na kulala,siku ikapita.
Kulivyokucha akasimama akaendelea tena kuomba kama kawaida,akitembea barabarani na kugonga vioo vya magari akiomba msaada.Siku hiyo jua la saa saba lilikuwa kali kupita kiasi, likamchoma mwilini,kutokana na kutokuwa na viatu miguuni lami ikawa inamuunguza lakini alijikaza,ilikuwa ni lazima aombe ili apate pesa na kula.Alipakumbuka nyumbani kwao Moshi mara mia mia, lakini hakuwa na nauli ya kwenda,akafika eneo lake la kuombea pesa ubungo mataa, kama anavyofanya akaanza kupita kila gari akigonga vioo akiomba msaada wa angalau shilingi mia akale.Akalipita DCM kubwa lililojaza abiria,akatembea mpaka kwenye Prado nyeupe kisha kulifikia gari aina ya ‘ALTEZA’ nyeusi ya kisasa yenye rangi nyeusi ya kung’aa yenye vioo vya rangi nyeusi pia.Hakuweza kuona mtu aliyekuwa ndani ya gari.
“Kokokoko..”
Gloria akagonga kioo cha gari huku akiwa amekinga mikono yake akiomba msaada,alitia huruma.Kioo cha gari kikashushwa!
“Naomba msaada Baba…sijala tangu jana,hata kama una shilingi mia naomba…”
Lilikuwa ni ombi kutoka kwa Gloria,akimtizama mwanaume mweupe aliyekuwa kwenye usukani,ni miaka mingi ilipita.
Maskini ya Mungu,hakujua kuwa ni Nickson Shayo mume wake wa ndoa.Ni Nickson mwenyewe baada ya kumtizama kwa kwa muda kidogo alimtambua,akampandisha juu mpaka chini na kupandisha kioo cha gari juu.
“Baba Sonia!si umsaidie kwani huna hata elfu moja hapo?”
Pendo alisema,hakuelewa lolote wala kujua kuwa ni Gloria.
“Sina”
“MIMI ninayo,wacha nimsaidie”
Pendo akaingiza mkono kwenye mkoba wake hapo ndipo Sonia aliyekuwa nyuma akawa amemkazia macho Mwanamke huyo aliyekuwa akiomba barabarani.
“Mamaaaaa”
Sonia akasema kwa mshangao.
Hapo hapo taa za kijani zikaruhusu,Nickson bila kusema lolote akaweka gia na kukanyaga mafuta akalitoa gari.
“Daad please stop the car,please Dad”(Baba tafadhali simamisha gari,Baba nakuomba)
Sonia aliumia moyo akawa anageuza geuza shingo yake nyuma,safari ya kwenda kufurahi na kula chakula cha mchana hakuhitaji tena,akapiga kelele kwamba gari lisimamishwe.
“Sonia,nini tatizo?”
“Naomba usimamishe gari”
“Nitasimamisha vipi gari hapa wakati hakuna paking,ili iweje?”
“Nimemuona Mama”
“Siwezi kusimama,Am sorry”
Kitendo cha kuongea ivyo Sonia akawa ameshika kitasa cha mlango,akafungua gari likiwa hivyo hivyo linatembea.Ilikuwa kama Mungu Nickson kuangalia ‘sitemirror’ za pembeni na kushuhudia kitendo hiko hatari, akaweka mguu kati,Sonia akatoka ndani ya gari kama mkuki.Magari yalikuwa yanaenda kwa kasi ya ajabu, yalikuwa yameruhusiwa, ilikuwa ni hatari kubwa mno.

Hati hati ya kugongwa na gari kwa Sonia ilikuwa ni asilimia tisini na mbili,ikamlazimu Nickson apaki gari pembeni na kumfuata Sonia nyuma nyuma,ilikuwa ni kama sinema ya kihindi.
“Mamaaa Mamaaaaa”
Sonia aliita baada ya kumfikia Gloria aliyekuwa kandokando ya barabara.
“Nawewe ni nani?”
Gloria akauliza.
“Mimi Sonia mwanao”
Hapo ndipo machozi yalianza kum-bubujika Gloria,akapiga magoti na kulia kwa sauti kubwa iliyojaa majuto,kila mtu aliyepita alilazimika kugeuza shingo yake.
“Mwa..nangu nateseka sa…na natese..ka mama yako”
“Mama nimekuja,nakupenda Mama simama twende nyumbani”
Sonia akasema kwa uchungu huku akianza kulia machozi,japokuwa alielewa ni kiasi gani mama yake alikuwa akitenda mambo mabaya miaka iliyopita,alijua ni kiasi gani alivyokuwa msaliti kwa Baba yake lakini hakutaka kumchukia kiasi hicho.
“Sonia,tuondoke”
Nickson akaingilia kati baada ya kutokea nyuma yake,hakutaka kumuangalia Gloria machoni akamvuta Sonia kwa nguvu.
“Dad niache,Dad niache”
“Siwezi kukuacha tuondoke,nakwambia tuondoke nitakuzaba makofi”
“Baba niache na Mama yangu”
“Soniaa,nisikilize mimi baba yako”
Mambo hayo yalitokea mbele ya Gloria,hapo ndipo alipozidi kulia.
Alijionea huruma na kujichukia mwenyewe.
“Na..omba unisameh..e Nickson”
“Nyamaza!sahau kabisa,nakwambia usahau wacha dunia ikufunze”
Nickson akamvuta mwanaye kwa nguvu,akamburuza mpaka ndani ya gari wakamuacha Gloria anawafuata nyuma nyuma akilia machozi na kuomba msamaha akitaka kurudi nyumbani.
“Gloria toka,usinigasi gasi mbona unakuwa hunielewi?sikutaki sahau kuwa namimi tena,nilikupenda sana lakini siwezi tena kukupenda”
Akiwa mkavu, Nickson aliyatamka maneno hayo huku akifungua mlango wa gari lake,akitaka kuingia ndani lakini Gloria alimkamata shati na kumvuta kwa nje,ilikuwa kidogo amkatie vifungo.Watu walikuwa wameshajaa wanashangaa kitendo hicho,kwa mara ya kwanza walidhani wenda kuna maigizo ya filamu yalikuwa yanafanyika.
“Wewe Malaya niache nakwambia,usinishike Gloria,utanichania shati langu…..”
Nickson hakutaka kuongea kitu kingine,akamsukuma Gloria mbali,akadondoka puu juu ya lami chali.
Akaingia ndani ya gari na kulitoa kasi.Tayari moyo wake ulibadilika na kuwa wa shetani, alimchukia vibaya sana kiumbe aliyeitwa Gloria kuliko kinyesi.Ndani ya gari kulijaa kelele Sonia alizidi kulia machozi huku akigeuka nyuma na kumtimzama mama yake aliyekuwa amelala juu ya lami,Pendo alikuwa amekaa kimnya,tangu amjue Nickson hakuwahi kumuona akiwa katika hali hiyo ya kukasirika,jinsi macho yake yalivyokuwa mekundu yalimtisha,kifua chake kilipanda juu na kushuka mapafu yake yakajaa hewa,midomo ikawa inamcheza kwa hasira.
“Daad”
“Shut up Sonia,I said shut up!”(Kaa kimnya Sonia,nakwambia kaa kimnya)
Nickson akaropoka kwa hasira tena kwa sauti kubwa iliyosindikizwa na ukali.

*****

Ndani ya gari ulizuka mtafaruku mkubwa kupita kiasi,Sonia hakutaka kuamini kuwa baba yake angekuwa ana roho ya kinyama kiasi hicho,haikuwezekana kuamini kwamba kitu kama hicho kingetokea,wakati mwingine alidhani ni ndoto na baadaye angeshtuka,Mambo yaliyokuwa yanatokea yalimshangaza,akabaki analia tu,akamtizama baba yake kwa macho yaliyojaa hasira.
”Dad i hate you,i hate you dad, sitaki kuamini kama unafanya mambo kama haya,kisa huyu mwanamke, ndiyo unamfanya mama yangu vile”
zilikuwa ni hasira zilizozidi kipimo chake,hata kama kungekuwa kuna kifaa cha kupunguza hasira kisingeweza kuzuia jazba za binti huyu.
Nickson akazidi kuendesha gari hakutaka tena kumsikiliza Sonia anayelia machozi,mambo yaliyokuwa yametokea hakutaka kuyawaza na kujutia kwa kitu alichokifanya.Mambo yote aliyaona sawa.Mpaka wanafika Samaki samaki bado Sonia aliendelea kulia kwa hasira,macho yake yakamvimba yakawa mekundu kupita kiasi.
”Tumefika shuka kwenye gari”
Nickson alimwambia mwanaye baada ya kufungua mlango wa nyuma lakini Sonia aliendelea kulia tu.Akainua shingo yake na kumtizama baba yake kwa macho makali yaliyojaa chuki.
”Nim..eshiba”
Sonia akajibu kwa kwikwi,isingekuwa busara ama asingekuwa ni baba yake mzazi angekuwa keshatoa matusi mengi yasiyokuwa na idadi kamili,alisikia kitu moyoni mwake kinamwambia ’hapana huyu ni baba yako mzazi’Sonia akaisikiliza sauti ndiyo maana akajibu kistaarabu.
”Sonia twende,sasa ushakuja mpaka huku itakuwa sio vizuri”
”Dad nimeshiba,nimeshasema”
Sonia akazidi kuweka mgomo akakataa katakata kushuka ndani ya gari,alichofanya Nickson ni kushuka na Pendo pamoja na mtoto wao Brenda wakanyoosha mpaka kwenye vyakula wakaagiza,lakini wakati wote Pendo hakuonesha furaha yoyote ile.
”Nickson unanipenda?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Pendo,Nickson akainua shingo yake hakutarajia swali kama hilo.
”Kwanini unaniuliza hivyo?”
Nickson akajibu kwa swali.
”Naomba unijibu kwanza”
”Ofcourse nakupenda na unajua hilo”
”Si umeona kitu kilichotokea leo?naamini ipo siku utarudiana na Gloria kisha utaniacha mimi najua unampenda sana Sonia alafu unamsikiliza mno, lakini nina uliza sina maana mbaya Nickson,kama utaamua kufanya hivyo tafadhali niambie”
Kijiko kilichokuwa karibu na mdomo wa Nickson kilichojaa chakula kikashushwa chini,lilikuwa ni jambo la kushtusha Nickson akanyamaza kwa muda akijaribu kutafakari mambo aliyoambiwa na Pendo,akamwangalia kwa macho yaliyojaa huruma,kuna kitu alikisoma machoni mwa Pendo ambacho hakikuwa cha kawaida,akashusha pumzi za ndani kwa ndani.
”Pendo, mimi nakupenda sana na nisingependa habari za Gloria tuziongelee naomba uyaache haya mambo kama yalivyo,nafikiri umenielewa”
”sawa”Pendo akaitikia kwa shingo upande.
Lilikuwa ni jibu ambalo halijanyooka kama swali lilivyotaka liwe,Nickson alimuweka Pendo njia panda.
Siku hiyo walikunywa na kula kisha wakachukua ’takeaway’kwa ajili ya Sonia,hao wakarudi ndani ya gari na kurejea zao nyumbani.
******

Gloria alizidi kuteseka akiwa kama ombaomba barabarani,kutokana na kukosa matunzo afya yake ikazidi kukongoroka akawa mwembamba mithili ya kijiti cha meno,uso ulikuwa umejawa na vipele alianza kutapika mara kwa mara na wakati mwingine alishindwa kutembea hata umbali wa mita kumi tu,kwa mambo yalivyokuwa yanamtokea aliamini kabisa yeye ndiye aliyejitakia,hakutaka kumlaumu mtu alibaki tu akilia machozi kila alivyokuwa akikumbuka mambo aliyokuwa akifanya,siku moja alikuwa akipita nje ya duka kubwa la vipodozi maeneo ya Ubungo lililoitwa M&K cosmetics.
Alivyopita mbele ya kioo cha duka hilo alijikataa,akatulia kwa muda akiwa anajitizama.Hapohapo alijikuta analia machozi,kilichomfanya aumie moyo ni jinsi uso wake ulivyoharibika kutokana na dawa za kichina alizokuwa anatumia kuweka sura yake sawa miaka mingi iliyopita.
”Wewe chokoraa embu toa usiku hapa”
Mwanaume mmoja mnene mwenye kitambi alifoka baada ya kumuona Gloria.
”Wewe nimekwambia toka eneo hili,nenda huko mbele”
”Kaka naomba msaada”
”Nenda msikitini,hapa sio mahala pake”
”Bosi Eddy achana naye huyo chokoraa njoo tumalizie kupiga hesabu”
Sauti iliyotokea ndani ikamtoa mwanaume huyo aliyekuwa anataka kumsukumiza Gloria mbali,akaingia ndani na kumuacha Gloria anatangatanga.
*****
Zaidi ya mara tano alishamuona Gloria Ubungo mataa lakini hakutaka hata siku moja kufungua kioo chake cha gari na kumpa hata shilingi mia moja yake,japokuwa alikuwa anamchukia kwa mambo mabaya aliyowahi kumfanyia hapo nyuma ata akadiriki kuingiliwa kinyume na maumbile lakini hakumuombea afe,alimuomba Mungu siku zote awepo hai ili aendelee kupata funzo na aonje joto la jiwe.

Siku moja Jumamosi aliwasha gari mpaka Ubungo maeneo ya Riverside nia yake siku hiyo ilikuwa ni kumuona Gloria.Nickson akapaki gari pembeni vizuri lakini hakushuka,akasubiri kama nusu saa ndipo alipomuona Gloria anatangatanga barabarani.kazi yake ikawa ni kumchora kila hatua anayofanya.
”Naomba,nisa..idie nina njaa”
Gloria alizidi kuomba msaada kila alipoliona gari mbele yake, akazidi kusogea mpaka kwenye Landcruiser v8 iliyopaki kando kando ya barabara kisha kugonga kioo cheusi,hakujua kuwa lilikuwa ni gari ya Nickson na alikuwa akichorwa.
Kioo kilizidi kugongwa Nickson hakutaka kukisusha alibaki tu akimtizama kwa hasira,pepo mchafu akawa amemkaba akatamani afungue gari ampige makofi lakini akamuonea sana huruma,alielewa fika kwamba jambo hilo lingempa kesi kubwa,akaamini kwamba angempa kofi moja angemuuwa.Hapohapo akawasha gari na kuliondoa kwa kasi.
****
”Mwanangu Nick,yule malaya anaumwa mno”
”Nani?”
”Si mkeo Gloria”
”Ndio najua anaumwa”
”Nakupa wiki,hiyoooo,Wiki hiyooooo,Mojaaa anakata moto yule”
Tito alikuwa ofisini kwa Nickson siku hiyo asubuhi anaongea akiwa anatia huruma tena ni kwa mara ya kwanza akiwa anaongea kwa simanzi,hali ya Gloria ilimtisha kupita kiasi akaogopa mno.
”Ndio,sasa unataka mimi nimsaidie nini?”
”Ah Nickson,wewe hujui kwani?itakuwa noma ujuwe bora umrudishe akafie huko kwao Moshi”
”Ah wapi”
”Usiseme ivyo Nickson,mpeleke kwao yule ohoo,mimi nakushauri vizuri yule si ulimtoa Moshi basi mrudishe hukohuko hapa anapata sana shida”
Ulikuwa ni ushauri kutoka kwa Tito kwa jinsi alivyoutilia mkazo na Nickson alivyokuwa anamheshimu rafiki yake akajikuta anamsikiliza, ikabaki kazi moja tu,ya kwenda Ubungo na kumchukua.
”Nanii Titoo”
Nickson akaita alivyoona Tito kafika mlangoni,ilionekana alikuwa ana jambo anataka kumwambia.
”Vipi?”
”Hivi kesi ya bosi Magugu imeishia wapi?”
”Kapigwa lidandasi,haijulikani lini atarudi ofisini bodi itakaa chini itafute bosi mwingine,nilimsikia Mheshimiwa Paul anasema sijui Konzo ndiyo awe bosi,hapa patakuwa hapatoshi yule mzee akiwa mkurugenzi”
”Konzo ndiyo nani?”
”Yule mzee mfupi Mweusi,ana kichwa kama madenge,ana kichogo hivi fulani kama wale Zena na Betina kwenye gazeti sijui la s……”
Kabla ya Tito kumalizia maneno yake Nickson alivunjika mbavu kwa kucheka,akapasua mbavu mpaka akawa anapiga piga meza,Tito alikuwa amemchekesha.
”Ha ha ha haha hahahahahahahahahaha…Tito eeh Hahaha nenda Bwana hahahahah Embu hahaha nenda nje”
Hata Tito alivyoondoka akabaki anaendelea kucheka.

Siku iliyofuata akaomba Ruksa ofisini kwamba anasafiri na pia akamtaarifu na Pendo juu ya safari lakini hakumwambia lolote kuhusu Gloria,siku hiyo asubuhi akafungua boneti la gari akawa anaangalia kabureta kama ina maji akachomoa dipstick akapima oil kama inatosha,akaweka kila kitu sawa. Kwa kuwa gari yake aina Landcruiser v8 ilitoka service muda mfupi uliopita,aliamini kwamba safari anayokwenda angefika mapema.

Akaingia ndani ya gari na kumuaga Sonia.
Haikuchukua hata muda mwingi akawa amefika Ubungo mataa akaweka gari pembeni,ikawa kama Mungu akamuona Gloria hapohapo, akamfuata.
”Gloria,twende kwenye gari”
”Nickso….”
”Ingia ndani ya gari”
Haraka bila kujifikiria akaanza kutembea taratibu mpaka ndani ya gari,ambapo cha kwanza Nickson alipita duka moja la nguo na kununua, akamvalisha Gloria.
”Nataka nikupeleke Moshi kwa wazazi,bado nakupenda Gloria nataka watupe tena baraka zetu,vaa nguo hizi”
Kwa Gloria lilikuwa ni jambo la kushtusha hakuamini hata kidogo,bado alikuwa ndani ya giza nene hakuelewa kichwani mwa Nickson kuna mahesabu gani.

*****


Gari aina ya Lancruiser v8 lililokuwa linaendeshwa na Nickson akiwa amembeba Gloria ndani kwa safari ya kwenda mkoani Kilimanjaro,lilizidi kuchanja mbuga, walifika Njia panda saa nane mchana,huko walipotoka hakuna sehemu waliyosimama zaidi tu ya Korogwe kujaza mafuta na kununua chakula,mahesabu ya Nickson yalikuwa yapo sahihi kwamba afike saa nane Mkoani hapo,hivyo ndivyo ilivyokuwa.

Ndani ya gari hakukuwa na stori nyingi zaidi ya Gloria akiomba msamaha, japokuwa Nickson alidai kwamba alimsamehe siku nyingi sana.Nusu saa baadaye tayari walikuwa wanakunja kona Mwika sokoni,hapo walikata kona na dakika tano walisimamisha gari nje ya nyumba ya Mzee Urio.Ulikuwa ni ujio wa ghafla,tangu safari inaanza Nickson hakuwataarifu.Mzee Urio alipoliona gari, kwanza alianza kujihami sababu hakuwahi kuliona gari hilo kabla,japo alielewa ni wageni wake.
”Mzee shikamoo”
Nickson alisalimia baada ya kushuka ndani ya gari lakini mzee Urio,hakuitikia salamu bado alionekana kumshangaa mwanaume aliyekuwa anamsalimia,alikuwa akivuta kumbukumbu ya wapi alimuona,kutokana na uzee.
”Eh Nickson,Ndiyo wewe Mwanangu?”
”Ndio mimi baba”
”Mbona ghafla ivyo?”
Mzee Urio akauliza kwa hamaki,akawa ana kazi ya kumtizama mwanamke mwembamba aliyekuwa anashuka ndani ya gari pia.
”Naona umekuja na mgeni,karibu nyumbani”
Mzee Urio akazidi kuongea,akamwangalia msichana huyu aliyekonda,hakujua kabisa kwamba ni binti yake Gloria.
”Baba mimi Gloria”
Kauli hiyo ikamshangaza sana Mzee Urio,akabaki ameyatumbua macho yake anamsaili akamwangalia kuanzia chini mpaka juu,akijaribu kuhakiki maneno aliyoambiwa lakini alijikuta anakataa.
”Gloria?Gloria gani?lakini sawa tu karibu kwetu Moshi,Nickson karibu ndani”
Bado Mzee Urio alikuwa ndani ya giza nene,hakuweza kuelewa lolote kuhusu Gloria mwanaye, bado aliendelea kuamini kuwa alikuwa ni mgeni wa Nickson kutoka jijini Dar es salaam,hatimaye akawakaribisha ndani wakaletewa chakula wakala na kushiba,wakati yote yanaendelea Nickson alikuwa ametulia tuli kama maji mtungini,akasubiri mpaka mambo yatulie na Mzee Urio aulize tena swali lake.
”Mwanangu,embu niambie vipi mwezako hajambo huko mjini?mbona yeye hakuja?”
Mzee Urio akazidi kuuliza,kauli hiyo ikazidi kumuumiza moyo Gloria,akaanza kumwaga machozi ni dhahiri kwamba alijua baba yake hakumtambua kabisa,aliumia moyo,machozi yakaanza kumbubujika mfululizo
mashavuji.
Nickson akabaki kimnya, sio kwamba swali hilo hakulisikia,alitaka alijibu Gloria mwenyewe aliyekuwa pembeni.
”Ba…ba ni mimi ni Gloria”
”Gloriaa?Gloria gani?”
”Gloria mwanao baba,mimi ni Gloria mtoto wako naomba unisamehe ba..ba nimekosea ulimwengu umenifu..nza vya kutosha.Nimekuaibisha san ana….”
Gloria alishindwa kumalizia kuongea, kwikwi ikamkaba akaanza kulia,Nickson akashindwa kuvumilia akahisi mashavu yake yanalowana na machozi yakadondoka chini sakafuni,ilikuwa ni kama picha ya kihindi.

Mambo aliyokuwa anayasema Gloria yalihuzunisha, hatimaye Nickson akashindwa kuvumilia akainuka na kutoka, akazama ndani ya gari ,jinsi alivyolizungusha isingekuwa utaalamu angeliingiza kwenye mashaba ya kahawa na migomba,akaliweka sawa na kilichoonekana hapo ni vumbi jekundu la udongo,Nickson akatokomea.

****
Hakuna aliyebisha kwamba Nickson alikuwa na mapenzi ya dhati kwa Gloria hata alivyowaeleza nyumbani kwao nini kilimpeleka Moshi wote walimuelewa,Mama yake alisikitika lakini hakuwa na namna ya kufanya.
”Mwanangu”
”Naam Mama”
”Pole na kila kitu,hayo ndiyo mambo ya dunia”
”Ahsante Mama angu”
”Sasa nawewe vipi,ulipima afya yako?”
Lilikuwa ni swali lingine kutoka kwa Mama Nickson akionesha hali ya wasiwasi.
”Ndio mama nilipima,hali yangu freshi kabisa”
”Kuna jambo nilikuwa nataka kukwambia”
”Jambo gani Mama?”
”Unamkumbuka Rukia?”
Swali la mama likamfanya Nickson akagande kidogo akaonekana kama mtu anayetafakari kitu fulani,akakumbuka vitu vingi na kuitikia kwa kichwa akimaanisha kuwa anamkumbuka.
”Ushawahi kuwasiliana naye?”
”Hapana Mama”
”Mtafute umuone mwanao,nilikutetea sana,mwanao anaitwa Paulina,alijifungua kwa njia ya operesheni,wazazi wake walikasirika sana,bila mimi na baba yako kukinga vifua sijui ingekuwaje”
Ilikuwa ni habari mpya kwa Nickson lakini hakutegemea kupata mambo kama hayo akabaki ameachama mndomo wake wazi.
Kitu kingine kilichomchanganya akili yake ni swala la Pendo Jonas, tayari alikuwa amezaa naye mtoto tena alikuwa ni mdogo.
”Sawa nipatie namba zake”
Nickson akafanya siri, swala hilo hakutaka kuliongea sababu angeonekana muhuni kwa mama yake alijua angesema habari za Pendo au kuzaa tena angeonekana hafai.
”Subiri kidogo”
Mama akasimama baada ya dakika moja akarudi na ’diary’ akamuonesha namba mwanaye.Hapo hapo Nickson hakutaka kupoteza muda akaipiga namba, alikuwa ana hamu sana ya kuongea na Rukia.Simu ikawa sikioni inaita lakini haikupokelewa akajaribu tena na tena.
”Mbona hapokei simu?”
Nickson akamuhoji Mama yake.
”Labda ujaribu tena baadaye”
Hazikupita dakika mbili simu ya Nickson ikawa inaita,ni Rukia ndiye alikuwa akipiga lakini alivyotaka kuipokea ikakatika,Rukia alibip,Nickson akapanda hewani.
”Halloo Rukia”
”Abee nani mwenzangu?”
”Mimi Nickson,Nickson Shayo”
”Nickson Shayo!nikusaidie nini labda?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Rukia likisindikizwa na sauti ya ukali kupita kiasi,Nickson akakohoa kidogo ili kukusanya nguvu mpya za kupiga saundi.
”Nahitaji kuzungumza nawewe al…tititi”
Simu ikakatwa hapohapo,Rukia alikata simu, picha ikaonesha kuwa hakutaka mawasiliano yoyote na Nickson.Hivyo ndivyo ilivyokuwa.
****
Tayari Nickson alikuwa baba wa watoto watatu:Sonia,Brenda na Paulina hilo halikuwa na ubishi,lakini Brenda bado hakufahamika nyumbani kwao kwani jambo hilo hakutaka kuliweka wazi kabisa,kilichomchanganya akili yake ni kitendo cha Rukia kutokupokea simu na siku mbili zilipopita mawasiliano yakakatika kabisa,Rukia hakupatikana simuni.
”Mama!Rukia hapatikani,sasa sijui itakuwaje?”
Nickson siku hiyo alimwambia mama yake.Wakiwa katika zizi la Ng’ombe.
”Cha kufanya wewe nenda Mwanza,ndio ukasuluishe kila kitu mimi nitakuelekeza kila kitu”
Mama akamshauri mwana.
”Mama,niende bila wewe sasa?au bora niende na Mjomba Mackdonald si unajua yeye ndiye mwenye busara?”
”Sawa hakuna neno”
”Kitu kimoja kwanza,inabidi niende Dar kesho, kuna vitu nikaweke sawa ofisini kisha yeye aje ili twende Mwanza”
”Yote sawa Mwanangu”
Kama taratibu zilivyopangwa na ndivyo ilivyokuwa, Nickson alianza safari asubuhi na mapema akitumia gari lake Lancruiser V8 kutokea mkoani kwao na katika hesabu zake alipanga saa tisa ya alasiri awe amewasili Ubungo mataa,alivyowasha gari na kuwaaga wazazi wake akapitia nyumbani kwa Mzee Urio ili kuwaaga.
Kwa aibu walimsalimia huku vichwa vyao vikiwa chini,waliona aibu kwa kitendo alichofanya mtoto wao Gloria.
”Mwanangu safari njema,lakini uwe unatukumbuka”
”Baba usijali undugu wetu upo palepale,mtaendelea kuwa wazazi wangu tu,siwezi kuwatupa”
Nickson aliwapa moyo wazazi wa Gloria lakini bado walijisikia haya.
Kwa moyo mkunjufu wakapeana mikono na Nickson akawasha gari lake, akaligeuza na kulitoa kwa mwendo wa kawaida.
Alivyokuwa njiani Mara kwa mara wazazi wake walimpigia simu kutaka kujua ni wapi alifika.
”Ndio mzee,ndio nipo hapa Korogwe….Mzee mbona ni mwendo wa taratibu tu.Sawa nitakutaarifu..hakuna shaka”
Nickson akakata simu, akabadili gia akazidi kusonga mbele.

Saa tisa na dakika kumi na saba ya alasiri ndipo Nickson alipowasili mataa ya Ubungo,alitabasamu kwa kufika kwake salama, akakunja kushoto kuelekea barabara ya Mwenge,baada ya dakika kumi alikuwa amewasili Sinza.
Akaweka gari nyumbani kwake.
”Daaad……”
Sonia aliita kwa furaha na kumrukia baba yake,wote wakafurahi, haikupita hata dakika moja akatokeza Pendo Jonas wakakumbatiana kwa bashasha wote wakaingia chumbani.
Kilichofuata hapo ni madenda kwa kwenda mbele,kila mtu alionekana amemmisi mwenzake,nguo ya Pendo ikavuliwa na akabaki kama alivyozaliwa, Nickson nayeye akatupa nguo zake harakaharaka na kuingia bafuni,kilichoendelea huko ni kitendo ambacho watu chini ya umri wa miaka kumi na minane hawaruhusiwi kufanya.
*****
”Darling,leo naenda bank kuchukua pesa kesho kutwa nitasafiri naenda Mwanza kuna mambo naenda kuangalia”
”Honey,nitakumisi sana majuzi tu umerudi kutoka Moshi leo tena”
”Ndio ivyo mpenzi wangu,sina jinsi”
”Sawa love,safari njema kwahiyo ndiyo utaenda leo bank?”
”Ndio Mamii”
”Usisahau basi ile laki mbili niliyokuomba”
”Hilo usijali,nitakuja nayo”
Nickson hakutaka kuweka wazi ni kitu gani kinachompeleka Mwanza,alielewa ni jinsi gani Pendo alikuwa ni mwanamke mwenye wivu na asiye elewa somo tena linapokuja swala la Nickson kuwa na mahusiano na mwanamke mwingine kiholela,ndiyo maana alimficha kuwa ana mtoto mwingine wa nje mbali na Sonia.
Baada ya kuagana, Nickson akatoka nje na kuwasha gari kwa nia ya kuelekea HAJREYMER NATIONAL BANK ili kupakua pesa za safari na matumizi ya nyumbani.
***
Mtaa wa Samora Avenue ulikuwa katika hali ya utulivu wa hali ya juu sana,hakuna hata mtu mmoja aliyekuwa yupo nje anatembea wala kusogeza pua yake,lilikuwa ni jambo lisilo la kawaida.Hakuna hata mtu mmoja aliyethubutu kupita hata nje,pembezoni mwa mtaa huo kulikuwa kuna benki iliyowekwa chini ya ulinzi mkali na majambazi waliokuwa ndani,ambao kabla ya kuingia walimwaga risasi hewani ili kusambaratisha watu,hata vilema siku hiyo walitupa magongo na kuchanja mbunga!Mtaa ukawa mweupe.
”Wewe dada jina lako nani?”
”Mi..mi naitwa Jesca..Naitwa Jesca”
”Jesca,naona una pete ya ndoa una mume,weka pesa humu ndani ya begi haraka kabla sijasambaratisha ubongo wako,fanya upesi”
Tayari majambazi walizama ndani ya ofisi ya Mama Mkurugenzi wakitaka pesa nyingine,ilikuwa ni kauli ya kutisha.Mwanamke mtu mzima aliyeitwa Jesca alivuta droo harakaharaka na kutoa maburungutu ya pesa akafanya kama alivyoambiwa.
Kama umeme begi likajaa pesa,majambazi tisa waliokuwa na silaa za moto waliweza kuwaweka wafanyakazi wote chini ya ulinzi pamoja na wateja wote waliokuwa wameenda kwenye benki hiyo kuweka na kuchukua pesa zao.
Kwao siku hiyo ilikuwa ni ndefu mno.

Sio ivyo tu, hata walinzi walikuwa mateka, tena mmoja wao alikuwa teyari amemwaga mkojo.
”Wewe simama”
Jambazi mmoja akatoa amri akimwambia askari aliyekuwa lindo asimame.
”Paaaaaaaaaa”
Mlio mkubwa wa bastola ulisikika,askari alikuwa kapoteza maisha yake hapohapo baada ya kupigwa risasi moja ya utosi,hakuomba hata maji,hapohapo alidondoka chali huku damu zikimvuja,hofu ilianza kutanda.
Majambazi hayo tisa yaliyojiziba sura zao baada ya kuona tayari wamepata pesa za kutosha,walitoka nje na kuachia risasi tatu hewani.Watatu wakaingia ndani ya Mark II nyeusi waliokuja nayo na wengine sita wakasimama katikakati ya barabara baada ya kuona Landcruiser V8 inapita wakapiga risasi moja hewani.
”Fungua mlango,fungua mlango”
Jambazi mmoja akaamuru huku akielekezea gari ya Nickson Mtutu, aliyekuwa safarini kwenda kupakua pesa,moyo wake ukapiga kwa nguvu, haraka akafungua mlango majambazi yakaingia ndani.
”Lets go,Lets go,Drive”
Nickson tayari alikuwa amewekewa bastola shingoni,akaweka gia na kutii amri hazikupita hata dakika mbili,ving’ora vya polisi vikaanza kulia,askari wakaanza kufukuzia Landcruiser v8 nyeusi,majambazi walianza kurusha risasi kwa mapolisi, wakawauwa polisi watatu.
Nickson alizidi kutetemeka, kazi yake ilikuwa ni kuendesha gari kwa kasi,tayari alikuwa ana kesi ya kujibu sababu kivyovyote vile polisi walijua gari hilo limebeba majambazi waliouwa wenzao.

****

KATIKA MAISHA yake hakuwahi kuiona bastola, zaidi tu ndani ya sinema za kizungu za kuigiza,leo hii ipo shingoni mwake na ndiyo maana alikuwa akitetemeka kwa kiasi cha kutosha,mbali na kutoijua sawasawa,alielewa endapo ataenda kinyume na majambazi wanavyotaka ubongo wake ukasambaratishwa vibaya sana.
Majambazi watano walikuwa viti vya nyuma na mmoja alikuwa yupo kiti cha mbele kushoto mwa Nickson,wote walikuwa wana silaha kali za moto tena zimekokiwa zinamtizama yeye,alichotakiwa kufanya ni kuendesha gari kwa kasi na kutii amri akiwa kama mateka.

Landcruiser V8 ambayo ilisadikika kuwa imebeba majambazi ilizidi kutembea kwa mwendo wa kilomita mbili kwa sekunde,wakapita barabara ya OHIO huku magari ya mapolisi yakiwa nyuma yao yakiwafukuzia.
Jinsi Maaskari walivyokasirika haikuelezeka,walishapoteza wenzao zaidi ya watatu,kwahiyo walikuwa na usongo.
Askari walizidi kupeana taarifa kupitia redio upepo.
”Afande Oscar,ova unanipata?”
”Ndio nakupata ova,vipi mpo wapi?”
”Ndio tupo tayari hapa tunawasubiri wapite kila kitu kipo sawa”
”Tupo nao hapa sambamba, wanajaribu kurusha risasi,mkipata chance rusheni risasi”
Maaskari walizidi kufanya mawasiliano kwa njia ya redio upepo,walikuwa tayari wamejipanga na mitutu ili gari la majambazi likipita walimiminie risasi endapo wataleta ukaidi.Msako huo uliendeshwa na Kamishna wa polisi wa wilaya ya Ilala, afande Araphat Malewo.Kila kitu kilipangwa kama ilivyokuwa.
”Nyoosha mguu Nyoosha mguu kijana,tuna safari ndefu bado”
Ilikuwa ni kauli kutoka kwa mmoja wa majambazi aliyekuwa kiti cha nyuma kashika mtutu,Nickson hakuwa na jinsi akaweka gia akakanyaga mafuta,akazidi kusonga mbele,kila kitu alichokifanya alimwachia Mungu sababu maisha yake yalikuwa kama kamali siku hiyo,kufa au kupona!
Katika hali ya kushangaza diffenda nyingine ya polisi ikatokeza mbele kwa ghafla,Nickson alipojaribu kuweka mguu kati ili kusimamisha gari, akapewa onyo kali kwamba asijaribu kufanya ivyo kwani angeuliwa, hakuwa na jinsi zaidi ya kuendelea kuendesha gari,akaligonga difenda la polisi na kuzidi kwenda mbele.

Hapo ndipo askari walipoanza kurusha risasi mfululizo, zikaanza kupasua kioo cha nyuma.Polisi wakazidi kurusha risasi zisizokuwa na idadi.
Ilikuwa ni kama kapata akili mpya baada ya kuwaona askari, ilibidi atumie mwanya huo ili kuinusuru roho yake,kama swala Nickson akafungua mlango na kujitupa nje.
”Paaa paa paa paaaa”
Kabla hajatua ardhini zilisikika risasi nne, mbili zilikuwa zimepita hewani na nyingine mbili zilitua tumboni mwa Nickson,askari mmoja aliyekuwa na hasira kama mbogo ndiye aliyefanya jambo hilo,akidhani ni mmoja wa majambazi.

Kufumba na kufumbua Nickson alikuwa chali amelishika tumbo, anahisi maumiviu makali huku damu nyingi zikiwa zinamvuja zikasambaa kwenye lami,anagugumia kwa maumivu makali.Maumivu aliyokuwa anahisi hakuwahi kuyapata tangu azaliwe,alihisi kizunguzungu kikali,kwa mbali aliziona diffenda zinakuja zikapiga misele askari wakashuka,bila kuuliza chochote wakamuwekea mguu shingoni.
”Tume..kukamata leo..utaeleza”
Hiyo ndiyo kauli ya mwisho,aliyosikia baada ya hapo aliona giza nene na kitu kama ukungu aliona mbele yake,akaikumbuka familia yake, hapohapo macho yake yakafumba.
*****
”Baby leo ivyoooooo? Vingapii? Vitatu leo nakupiga daban,wazungu wanasema non-stop”
”Baby nawewe mbona fujo?”
”Nakwambia kweli,tukitoka hapa tunaenda kwa wananjenje pale Mlalakuwa.Wanakuja pale, shimo limetema nina pesa Punda habebi,alafu leo twende alkapela,kila siku napiga vesi vesi vesi tu,leo nyama kwa nyama”
Maneno hayo yalimtoka Tito,
Kitandani alikuwa amelala msichana wa makamo mwenye rangi nyeusi ya kuteleza,alikuwa ni msichana wa kidigo mwenye macho makubwa na lips nzuri zilizonona,katika wasichana arobaini aliowahi kutembea nao alikiri kuwa Tausi ni kiboko yao, sababu alidai kwamba ikulu yake ina hali ya ujoto alafu ni ndogo,inabana.
”Tito,mbona huwa kila siku unanisifia sana?”
”Ngoja nikwambie ukweli,wewe ni mtamu kama sijui kitu gani maana nikisema asali unazidi,Damsugare una ifahamu?”
”Hee!Ndio nini hiyo tena?”
”Ile mashine ya kufanyia usafi,kuna kipindi nilienda Sweden,ndiyo inavyoitwa ya kusafishia makapeti basi naniii yako nikichomeka bunzi langu nanii yako inavuta kam….”
Tito akakatishwa maneno yake,Tausi akamvuta kwake na kuanza kulana denda.
Hapohapo nguo zikatolewa taratibu vifungo vya Tito vikafunguliwa,vest ikavuliwa, Tausi akashuka chini na kutoa jeans ya Tito na boxa ikatupwa mbali,kitu cha kwanza Tausi kufanya ni kushika mwiko wa Nickson akauweka Mdomoni,hapo ndipo Tito alipohisi mambo yanaharibika akabaki tu ameachama mdomo wake,nayeye hakutaka kuwa gogo akapeleka mkono wake mpaka kwenye maziwa juu ya chuchu za Tausi akaanza kuzitomasa taratibu sana,
akamvuta karibu akamuweka chali,alivyoona anapata shida akaamua kuitoa nguo ya juu ya Tausi na kuanza kumnyonya maziwa kwa fujo huku mkono wake taratibu ukiwa unapita chini ya ikulu,
akakifikia kitu kilaini cha juu na kuanza kukipalaza,hapo ndipo msichana huyu Tausi alipohisi kupagawa.
”Griiiii griiiii,Griiii Griiiiii”
Simu ilisikika ikiita kutokea mezani lakini Tito akaipuuzia,alianza kujilaumu ni kwanini hakuzima simu kwenye swala hilo zito analotaka kulifanya,akabaki tu anasonya na kuzidi kumpapasa Tausi kila sehemu ya mwili wake,akamchojoa nguo zote na kuipanua miguu yake.Simu ilizidi kuita ikawa kero kwake.
”Baby ngoja nikazime simu,maana ishakuwa kero”
Hiyo ndiyo sentensi aliyosema Tito,akaachana na Tausi na kumpiga Denda,akatembea mpaka mezani akiwa uchi wa mnyama.
Kabla ya kuizima akatizama kioo cha simu akaona jina ’NICKSON’alivyotaka kuikata na kuizima moyo wake ukasita,akaipokea na kuiweka sikioni.
”Oyaa!Nickson vipi tena? mbona unataka kuharibu starehe za watu mwamba?enhee una shida gani mkali wangu?”
”Hallooo”
Upande wa pili wa simu ukasikika ukisema,Tito akashtuka sababu sauti haikuwa ya swaiba wake.
”Nickson”
”Hapana,hapa ni Hospitali ya Mwananyamala naomba uje mara moja haraka iwezekanavyo”
”wewe nani?”
”Tafadhali naomba uje”
Mashine ya Tito hapohapo ikasinyaa,habari hizo zilimtia mashaka kupita kiasi,alihisi kama joto mwilini mwake, kengele nyekundu ilianza kugonga kichwani kwamba kuna jambo lisilokuwa la kawaida limetokea.
Bila kuuliza chochote akatembea na kuchukua boxa yake chini, akaiweka mwilini akavaa harakaharaka kama umeme.
”Baby vipi?”
Tausi akauliza alivyoona habari inabadilika.
”Nakuja nisubiri humuhumu chumbani”
Hiyo ndiyo ilikuwa kauli ya Tito huku akitembea na kufunga vifungo vyake vya shati baada ya kuvaa jeans yake,akashuka ngazi harakaharaka mpaka kwenye parking za magari na kuingia ndani ya gari lake aina ya Rav 4 akaanza safari ya kwenda hospitali ya mwananyamala.
”Embu, nimekumbuka kitu,ngoja nimpigie Pendo nataka nijue kitu gani kinaendelea”
Tito akajisemea, hapohapo akaenda hewani.
”Chaurembo!vipi hali?upo wapi?”
”Tito hata salamu best,alafu mbona unaongea harakaharaka ivyo,ushafumaniwa nini?”
”No sio,kwanza upo wapi?”
”Nipo nyumbani,vipi?”
”Nickson yuko wapi?”
”Ametoka asubuhi hii,kwani wewe haupo naye?”
”Basi..basi.. basi,usijali nitakupigia”
Tito akakata simu,alichotaka kukijua aliamini kuwa Pendo haelewi lolote,nusu saa baadaye akawa amefika hospitali ya mwananyamala.
Mtu wa kwanza kukutana naye alikuwa ni Delphina Magombe,Wakili msaidizi,hali aliyomkuta nayo alishindwa kuelewa.
”Kuna nini?”
”Nickson kapigwa risasi”
”Whaaaaaat?”(nini)
”Siriazi!ana hali mbaya sana,tumuombee”
”Hapana,ilikuwaje?mbona sielewi Delphina”
”Ndio ivyo,ni stori ndefu lakini kwa jinsi nilivyoelezwa na madaktari sidhani kama kuna matumaini”
Tito alijikuta ananyong,onyea,alimtizama Delphina mara mbili mbili kama mtu asiyeamini kitu anachoambiwa na alitaka kujua zaidi nini kimetokea,isingewezekana hata kidogo kuamini habari hizo moja kwa moja.
”Imekuwaje?Mbona sikuelewi Delphina”
”Amepigwa risasi na maaskari,Mungu amsaidie huko alipo,yupo kwenye chumba cha operesheni madaktari ndiyo wanafanya jitihada za kutoa risasi tumboni mwake”
”Kwanini alipigwa risasi?”
”Yaani kwa jinsi nilivyoelezwa na maaskari ilikuwa hivi,Wale maja….”
Kabla ya Delphina kumalizia maneno aliyotaka kuongea,Madaktari waliokuwa chumba cha upasuaji wakaanza kutoka ndani ya chumba hicho mmoja baada ya mwingine.
Delphina akaruka kama simba na kumvaa mmoja wapo.
”Daktari vipi?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Delphina huku akimtizama dokta machoni.
”Subiri kwanza”
”Nisubiri nini sasa?”
Kupitia macho ya daktari,Delphina alijifunza kitu kwamba hakukuwa na habari nzuri.
”Nasikitika kuwaambia kuwa tumejitahidi kadri ya uwezo wetu lakini hatukufanikiwa….”


 Jinsi maaskari walivyokuwa na hasira haikuweza kuelezeka kiwepesi,matukio ya ujambazi yalivyotokea siku chache zilizopita na mambo ya uvamizi wa benki ulikidhiri na ndiyo maana hawakutaka kuwalazia damu majambazi walitokea kuvamia benki ya HAJREYMER dakika chache zilizopita.
CRDB tawi la chanika ilitokewa kuvamiwa na mapolisi kumi na moja walifariki dunia papohapo, baada ya majambazi kuwapiga risasi,hiyo iliwafanya wapate hasira zaidi na wapadishe mori.Na ndiyo maana mpaka Inpecta Cholo alikuwa kwenye msako huo ndani ya difenda iliyokuwa inaendeshwa na Afande Gadagada alitaka kwenda nao sambamba,operesheni iliendeshwa mbiombio kuliko siku zote.Kila kitu kilipangwa kijasusi na askari walikuwa radhi kufa au kupona,ndiyo maana walijitolea kwa hali na mali wakiwa tayari na mitutu yao wameiweka kariakoo katikati yaani, wameizingira.
Kwa jinsi mipango ilivyoenda,waliamini kwamba isingewezakana hata kidogo kwa majambazi hao kuwatoka.
Katika watu waliokuwa na hasira ni koplo Hussein,mdogo wake ambaye alikuwa ni mlinzi katika benki ya CRDB tawi la chanika alipigwa risasi saba kifuani,Koplo Hussein hakuwa katika msako wa majambazi tu, bali alikuwa akitaka kulipa kisasi.
Na ndiye alikuwa ndani ya diffenda ya nyuma anakimbizia Landecruiser v8 akiwa amejawa na hasira kupita kiasi, bastola yake ipo mkononi.Kitendo cha kumuona mtu ametupwa kutoka kwenye gari hiyo,aliachia risasi nne bila kuuliza.
“Afande stop”
Ilikuwa ni kauli kutoka kwa Afande Kibengele,akijaribu kumzuia mwenzake asizidi kutoa mashambulizi.Haraka wote wakatua ardhini wakatembea mpaka kwa mtu waliyehisi ni jambazi kitu cha kwanza kukifanya afande Cholo alikabwa na hasira akamfuata Mwanaume aliyempiga risasi akamuwekea mguu shingoni kwa nguvu.
“Kachakacha,paaaa”
Bastola ilivyokokiwa ikafyatuliwa kwa nia ya kumpiga Nickson utosini ili wamtoe uhai wake,isingekuwa Afande Kibengele kuupiga mkono wa Afande Hussein basi ubongo wa Nickson ungekuwa juu ya lami.
“Afande punguza hasira”
“Hapana,siwezi”
“Huyu jambazi anahitajika akiwa hai,inabidi ajibu mashtaka..Afande Morio embu uliza kama wameipata Landcruiser ya majambazi wengine?”
“Sawa wapo njiani”
Kwa jinsi walivyomtupa Nickson ndani ya diffenda kama mzoga ni dhahiri kwamba walidhani ni jambazi sugu.Nickson hakuwa na fahamu zozozte alikuwa nusu mfu tayari,alipigwa risasi kimakosa,damu nyingi sana alipoteza mwilini,akapoteza fahamu zake zote.Kila askari alimuangalia kama kinyesi na walijawa na hasira na kujipongeza kwa ushindi wa kumkamata jambazi.Lakini kati ya mmoja wa mapolisi alionekana akimuangalia Nickson kwa umakini,akamtizama.
“Jamani, huyu sio Nickson!?”
“Nickson?Nickson yupi?Nickson Mwaduma au?”
“Nickson Shayo,mwanasheria”
Kila mtu alimtizama askari huyu ambaye alisogea karibu na kumuangalia mtu huyo aliyedai kama ni Nickson,kitu cha kwanza kukifanya ni kuingiza mikono ndani ya suruali,akakutana na kitambnulisho.
“Mungu wangu”
“Nini?”
“Huyu ni Nickson Shayo,hapana”
Afande Mwicheche bado hakutaka kuamini kuwa Nickson alihusika na mambo ya ujambazi,hapohapo alimtafuta Delpihina Magombe,mfanyakazi mwenzake na Nickson huyu alikuwa ni ndugu yake na ndiyo alitaka kumpa taarifa juu ya kilichotokea.Taarifa hizo zilimshtua sana mwanadada huyo, akaacha kula chakula.
“Mko wapi?”
“Tunaelekea Mwananyamala hospitali,tafadhali naomba uje jaamaa ana hali mbaya sana”
“Nakuja sasa hivi,nipe dakika tano”
Walivyofika hospitali ni kweli.Hali ya Nickson Shayo ilikuwa mbaya kupita kiasi,risasi zilikuwa zimepenya kabisa na kutoboa utumbo,haikuwezekana hata kidogo kupona,labda tu ingetokea miujiza ya Mungu, hivyo ndivyo walivyosema madaktari wa hospitali hiyo.

Hapohapo wakatafuta ndugu wa karibu ndipo wakampata Tito.
kila daktari aliyemuona Mgonjwa huyo alitingisha kichwa,Nickson aliingizwa ndani ya chumba cha operesheni akiwa tayari kapoteza lita mbili za damu.Katikati ya operesheni mashine ya mapigo ya moyo ilianza kupiga kelele kisha kutulia.
“Dokta Vipi?”
LILIKUWA ni swali kutoka kwa Dokta Kandege,huku akionesha hali ya kuchanganyikiwa.
“He is gone”(Amefariki)
DOKTA Ikram akajibu huku akitoa kitu kama ‘mask’ puani mwake.Akatoka nje.
****
Alivyotoka tu,alifuatwa hapohapo na kukamatwa mkono na Tito,akajaribu kusema kilichotokea.
“Dokta embu ongea kiume,acha gozigozi bwana”
Tito aliongea kwa jazba huku akiwa karibu kabisa, sentimita moja pointi tisa mdomoni mwa daktari.
“Mgonjwa wenu amefariki dunia,hatupo naye tena duniani”
Tito wakati wote alidhani wenda anaota ndoto mbaya ya kutisha ambapo baada ya muda mfupi angeshtuka,lakini haikuwa ivyo.Maneno aliyoambiwa na daktari yalipita ndani ya ngoma zake za masikio na kugota kabisa kwenye moyo wake,akaganda kama barafu.Taarifa alizosikia zilikuwa za kutisha.
“Una..una una, se..ma kwamba?”
Akaongea kwa kigugumizi.
“Naomba mnipishe kidogo”
“Dokta embu subiri kwanza”
Hata siku moja Tito asingekubali kwamba kuna kitu kinaitwa kifo tena kwa rafiki yake wa karibu,Delphina Magombe aliyekuwa karibu alisikia kila mazumgumzo,yeye alibaki kulia machozi ya kwikwi,alishaelewa nini maana yake.
“Nick….soooooooooooon uwiiiiii”
Zilikuwa ni kelele kutoka kwa Delphina huku akiserereka chini na ukuta,akawa analia tu.Tito alikuwa amemkuda koti daktari.
“Dokta,Dokta,rafiki yanguu yangu yuko wapi?”
“Kijana embu niachie,utanichania koti langu”
“Nooo,Noooo…..RAFIKI YANGU AMEFARIKI HAIWEZEKANI HATA KIDOGO”
“Ndio hivyo ndiyo kazi za Mungu,lazima tukubali kuwa kifo kipo,tafadhali naomba niachie”
Tangu Tito azaliwe,hakuwahi kusikia uchungu kama siku hiyo,bado hakuamini kuwa swaiba wake Nickson kafariki dunia.
Kabla ya kumalizana na daktari akaona mlango unafunguliwa machela ikatolewa,Tito akakiendea haraka, bila kuuliza chochote akafungua shuka la bluu,akahisi kuishiwa nguvu alivyoiona sura ya Nickson imevimba,ameyafumba macho yake.Tayari alikuwa amefariki.
“Nick..Nickso...n embu amka ndugu yan..gu wake up son,amka mwanangu,wake up my boy...bado haujafa bwana,embu amka acha masi..hara aroo”
Tito aliongea kama mwendawazimu,madaktari wakamtoa pembeni,machozi yalikuwa teyari yanamtoka,akachuchumaa bila kupenda,mikono kichwani.
Kamasi lilimtoka likapita mpaka mdomoni mwake akaanza kulia kama mtoto wa miaka miwili,hakuwa mwanaume tena.
“Nicks..on Nick...son..sasa umeniacha na nani ndugu yangu..Embu niambi...e eeeh swai..b nitakunyw...a na nani po,mbe unadhani?…. Mb..ona umeo..ndoka m..apema kiasi hi..cho?kwanini hukujikaza sa..sa kiume?”
Tito hakuweza kujikaza kisabuni,akalia kupita kiasi alitia huruma.Maneno aliyoambiwa na daktari alidhani bado ni ndoto na baadaye atashtuka, mbali na hapo alitamani iwe hivyo.
Manesi waliopita pembeni na wao walijikuta wakidondosha machozi,walimuhurumia sana kijana aliyekuwa akilia mfululizo mpaka kamasi zikawa zinamtoka,yupo chini anapigapiga malumalu.
“Nick...on,umeniacha na nani,mshkaji wako….”
Kilio hakikukoma.Huo ndiyo ukawa mwisho wa Nickson Shayo Duniani.
****
Hakuna mtu aliyeweza kuamini kwamba Nickson Shayo amekuwa marehemu, bado waliamini ni sinema ya kuacti,watu wengi walijazana Sinza nyumbani kwake,wazee kwa vijana walilia na kuomboleza siku hiyo huku jeneza likiwa katikati ndani ya korido.
Pendo Jonas alizimia mara mbili kila akizinduka alizimia tena,alimuwaza mtoto mdogo Brenda aliyeachiwa na marehemu,lakini kilichomshagaza ndani ya msiba huo hakuna hata ndugu mmoja wa karibu aliyemjali.
Kila mtu alimtaja Gloria,kuna kitu alijifunza lakini alitulia na kubaki kulia na moyo wake,uchungu aliousikia haukuwa na kipimo chake.Hakuna mtu aliyelia sana kama Sonia,macho yake yalimvimba kila mtu alimshika na kumtuliza lakini haikusaidia chochote.Mwisho wa siku walikubali kilichotokea na Costa mbili zikatafutwa,kwa jinsi alivyopendwa na watu zilikodiwa tena costa nyingine kwa ajili ya heshima ya mwisho na kwenda kumpuzisha marehemu Nickson katika nyumba yake ya milele.
Saa tisa Alasiri safari ya kwenda mkoani Kilimanjaro ilianza na siku zote ndivyo ilivyokuwa kwamba ‘Mchaga hazikwi ugenini” saa moja kamili kesho yake, Msiba ukafika kijijini Mwika.
Mama shayo akajigalagaza chini kwa kilio, hakutaka kuamini kwamba Mwanaye kipenzi amenyakuliwa na Mungu.Isingewezekana hata kidogo kwa umri wa miaka thelathini na sita Nickson afariki,lawana zote alimtupia Mungu kwa jambo alilolifanya.
“Mama usilie,ndio kazi ya Mungu”
Mzee Mmoja aliyeitwa Kimarisa,alimtuliza Mama Nickson.Lakini jitihada zake hazikuzaa matunda, alikuwa ni kama ameuwasha moto.Gloria akalia mpaka kuchanganyikiwa,hata yeye aliumia moyo.
Baada ya ibada kukamilika,na kila kitu kwenda sawa.Mzee mmoja akasimama,kuongea.
“Marehemu ameacha,watoto wawili.Mmoja Sonia na Paulina,pia ameacha mke mmoja”
Kauli hiyo ilimshtua Pendo Jonas,mtoto aliyezaa na Nickson hakutambulika.Kulikuwa kuna kila dalili ya jambo baya kutokea mbeleni.

*****
“Pangala”
Glasi ilidondoka na kupasuka chini.
“Rukiaaaa”
“Abee Mama”
“Vipi huko jikoni?”
“Hapana Mama,nipo sawa”
Mbali na kudondosha kikombe lakini hakikumjeruhi mahali popote pale.Moyo wake ulienda kwa kasi kupita kiasi,akahisi kuna kitu kisichokuwa cha kawaida.Haraka akaingia chumbani na kumuangalia mwanaye ambaye alikuwa akisumbuliwa na maralia kali.
“Nasra...Nasra mwanangu Paulina...”
Rukia akazidi kumuita mwanaye akitumia majina yake yote mawili, huku akimsogelea,mtoto wake alikuwa kimnya katulia.Taa nyekundu ilianza kuwaka kichwani kuwa mwanaye tayari amefariki,kila alipozidi kupiga hatua ndipo mapigo yake yakazidi kupiga sana.
****

“NOO HATUKUTAMBUI,MIMI NDIYE MJOMBA WA MAREHEMU”
“Sijakataa baba yangu, lakini marehemu nimezaa naye mtoto”
“Hata kama.Sisi tutajuaje kama mlikutana kichochoroni huko akiwa amelewa mkafanya vitu vyenu,alafu nyie wanawake wa siku hizi mkiona mtu ana mali kidogo basi mnajitegesha”
“Alinipenda mwenyewe”
“Basi sikia naona labda hunielewi hapa utaondoka,tena leo hii.Hakuna cha nywii wala nywii”
Jibu hilo lilivyotolewa tu,Pendo Jonas aliketi na kushindwa kuendelea kujibishana na Mzee Bobu Nyange.Seble nzima ilijaa sura za wazee tupu,kilikuwa ni kikao cha kugawa Mirathi baada ya siku arobaini kuisha.
Na katika mikakati ya kugawa vitu vya Marehemu Nickson, Pendo Jonas hakuambulia hata kikombe na alikuwa ameachwa na mtoto mdogo aliyehitaji malezi mazuri,muda wote alivyokuwa amekaa kitini machozi yalikuwa yakimtoka.Mbali na hapo hata Gloria alimkandia, akidai kuwa mali hizo walichuma yeye na Marehemu Nickson,kutokana na hali ya udhoofu aliyokuwa nayo kila mtu alikuwa upande wake.
“Ndi..o ivyo mimi na marehemu tulichuma hizi mali zote,tukajenga hii nyumba sote,tulitoka mbali sana”
Gloria aliongea akiwa bado ana afya mbaya,alikonda sana, mabega yalikuwa yamempnda juu.
“Kwahiyo huyu binti mimi simtambui hata kidogo”
Gloria alizidi kupigilia msumari.
Hilo ndilo suluisho lililofanyika,Pendo Jonas na Mwanaye Brenda hawakutambulika,hakukuwa na jinsi nyingine ya kupangua mambo yaliyokuwa tayari yamepangwa na wazee hawa wa kichaga.
*****
Jukumu la kumlea Sonia Nickson Shayo,akalivaa Dustan.Na ndiyo ivyo kabla ya marehemu Nickson kufariki aliandika kila kitu kuhusu mali zake na alikuwa navyo Dustan,mwanasheria mkuu.Kipindi Nickson anafariki hakuwepo barani Afrika.
Alisafiri kikazi na alisikitika sana kupokea habari hizo akiwa Carlfonia nchini Marekani.Na ndiyo maana alivyotua Mwalimu Nyerere akaunga ndege Nyingine iliyompeleka K.I.A mkoani Kilimanjaro.Akafika mpaka Mwika,kwenye kaburi alilozikwa rafiki yake kipenzi na kuweka taji ili kumpa heshima ya mwisho.
“Nitahakikisha maneno uliyoniambia nitayafanyia kazi,tumekuwa kama ndugu sasa.Mungu ailaze roho yako pema peponi”
Aliongea Dustan akiwa pembeni ya kaburi la Nickson,akajikuta machozi yanamlenga akaweka ishara ya msalaba na kuweka shada lingine juu ya msalaba,kisha akaenda mpaka kwa Mzee Shayo na kuwapa pole.
Japokuwa wazazi wa Marehemu walimshauri alale lakini hakukubali.
“Mama,nitakuja siku nyingine lakini leo kulala Moshi sitoweza,inanibidi nikamalizie viporo nilivyoacha huko.Usijali kila kitu kitakuwa sawa,Wazee wangu”
“Basi kula hata chakula”
Hapo Dustan hakuweka kipingamizi.Akala na kushukuru,saa kumi na moja jioni alikua angani kurejea jijini Dar es salaam,dakika hamsini zilikuwa nyingi, ndege ikawa imeweka matairi yake Mwalimu Nyerere.Dustan akawa kama mlezi wa Sonia,jambo la kwanza kulifanya ni kumtoa wasiwasi na kutaka wazoeane.
Kila jioni ilikuwa ni lazima afike Sinza nyumbani kwa marehemu na kuongea na Sonia,baada ya siku nne wakawa marafiki.
“Shikamoo Anco”
“Marahaba,vipi hali Sonia?”
“Nipo salama,ngoja nikueletee Juisi”
“Pumzika mwanangu,Mama yupo?”
“Yupo,lakini amelala”
“Basi mwache apumzike”
“Sasa mwanangu,Nimekutafutia shule”
“Shule?”
“Ndio Sonia,kabla ya kukupeleka nataka nikuulize kama upo tayari kwenda,maana sio hapa tena”
“Wapi?”
“Ulaya,Europe ni kama College tu ukimaliza huko baada ya miaka kadhaa,nitaangalia ustaarabu mwingine shule ikiisha,lakini sasa hivi wacha tuongee haya,vipi utaenda?”
“Embu nieleweshe vizuri Anco”
Sionia akataka kujua zaidi.Dustan akaanza kumueleza kila kitu kinagaubaga.
“Huko utasoma mambo ya LAW itakusaidia ukipasi unaingia Level nyingine”
“Law mimi siwezi,mimi ndoto zangu nilikuwa nisome procurement,sasa itakuwaje?”
“Sawa,usijali lakini wakati mwingine ni lazima tuangalie future yako,mimi ninataka ufanye Law nina maana yangu kubwa tu,sasa hivi hutojua.Hata Marehemu baba yako alikuwa akipenda sana wewe usome Law,nadhani unajua hilo,sina uhakika kama alishawahi kukwambia”
“Alishawahi kuniambia,sio mara moja”
“Basi huko alipo atafurahi sana”
Sonia hakuwa na tatizo juu ya hilo.Kisomo kikamuingia kichwani akakubali.
“Kabla sijasahau ni nchi gani Anco?”
“Ulaya,Europe”
“Ulaya ni kubwa,hilo ni bara.Ni nchi gani hiko chuo kipo?”
“Sweden!”
****
Nchi za Scandnavia kama Germany,Norway,Denmark na Sweden hawakuwa warahisi kutoa viza.Kipindi cha nyuma Waafrika walipewa viza na wakaishia kutokomea hukohuko na ndiyo maana viza zao kutoka ulikuwa ni mlolongo mrefu.
Dustan alijaribu kupigiana nao kelele lakini hawakutaka kuwa waraisi,kila siku walipigwa kalenda.Asilimia zilikuwa kumi za wao kupata viza ya kwenda Nchini Sweden.
“Your visa has been denied Sonia,you have to apeal”
Sonia alikuwa amesimama nje ya kidirisha,anapewa jibu hilo kutoka ubalozini,akiambiwa kuwa hana vigezo vya kuomba viza,ivyo ajaribu tena kuandika barua nyingine.
“How?”(kivipi)
Sonia akataka kujua zaidi.
“Seat there and read this letter very careful”(kaa pale soma hii barua kwa umakini)
Akagundua kwamba barua ilimtaka apeleke mpaka barua iliyoandikwa na Dustan kama mdhamini wake pamoja na 'bankstatement',ikiambatanishwa na barua ya chuo anachoenda huko Sweden.Hakutaka kuendelea kusoma zaidi akampigia simu Dustan na kumueleza kila kitu kilivyoenda.
Hawakukata tamaa,simu ikapigwa Stockholm Univesity,barua ikatumwa kwa email.Ikapatikana,Dustan akaandika barua kama mdhamini.Akaenda bank na kupewa 'bankstatement',kila kitu kikawa sawa.Baada ya siku saba Viza ikawa imetoka.
***
Hakukuwa na muda wa kupoteza,walikata tiketi ya shirika la ndege kubwa KLM, ambapo wangebadilishiwa Amsterdam na kupanda ndege nyingine ingewapeleka mpaka uwanja wa ndege Arlanda.Ndege ilitarajiwa kuondoka Jijini Dar es salaam usiku wa saa sita,siku ya Jumatano March 04.

Saa moja jioni walikuwa tayari wamefika.Dustan alitaka kwenda naye mpaka Sweden,alitaka kumkabidhi Sonia mikononi mwa walimu,hapo ndipo angeamini kuwa Sonia yupo salama.Kama mambo yalivyopangwa na ndivyo ilivyokuwa.Walifika Amsterdam saa mbili ya asubuhi kesho yake na kushuka ndani ya ndege ili wabadili nyingine.Muda wote Sonia alikuwa amejikunyata,baridi lilimpiga sio masihara.
“Saa ngapi tutakuwa tumefika anco?”
Hapo ndipo Dustan akagundua kuwa Sonia anapigwa na baridi,jinsi alivyokuwa amejikunyata kila kitu kikawa wazi.Ikamlazimu anunue koti hapohapo na kumfunika.
“Baada ya masaa mawili,Hapa tutasubiri mpaka saa nne tutaingia boarding pass,tutaondoka zetu”
“Kumbe ni mbali?”
“Sio sana, kama Marekani”
Stori zikaendelea,hatimaye muda ukafika.Wakaingia ndani ya shirika la ndege ileile KLM ,baada ya dakika tano ndege ikaanza kuchana mawingu.
****
Hakuna hata mzungu mmoja aliyeweza kukubaliana na hali hiyo,kwamba Africa kuna wasichana wazuri kama Sonia,tena nchi isiyojulikana, Tanzania.
Sonia alifanikiwa kugeuza shingo za wazungu wakimtizama lakini waliogopa wakidhani kwamba mwanaume aliyekuwa anatembea naye pembeni ni mume wake,hilo waliliheshimu na ndiyo maana hawakutaka kumbugudhi Sonia.
“I need a taxi”(Nahitaji taxi)
“Where are you heading my friend?”(Unaelekea wapi rafiki yangu)
Dereva alimuuliza Dustan huku macho yake yote yakiwa kwa Sonia,uzuri wake ukamzuzua.
“Stockholm,Stockholm university”
“Okay my friend,i will charge you 400 cronna”
“Can I give you us dollar?”
“Yeah,sure”
Mizigo ilipakiwa ndani ya taxi na wakaanza safari dakika hiyohiyo.Ndani ya lisaa limoja wakawa wameingia mjini Stockholm.
Muda wote Sonia alikuwa amejikunyata anahisi baridi kali,koti alilovaa halikuzuia chochote.
“Anco kuna baridi sana”
“Pole sana,ngoja nitakutafutia koti lingine,alafu umefika kipindi kizuri,baridi ndiyo linaishia”
“Anco,kwani wewe ulishawahi kuishi huku?”
“Kutokana na mambo ya kazi yangu,huwa nazunguka zunguka kila mahali,kutetea watu.Hii nchi nilikuja miaka kama mitano iliyopita”
Kila kilichoulizwa na Sonia kilijibiwa kiufasaha,mpaka Taxi inafunga breki nje ya chuo kikuu cha Stockholm Sonia hakumaliza maswali yake.
Dereva taxi akapewa ujira wake na kuondoka zake.

Kwa kuwa Ujio wa watu hao wawili ulitegemewa haikumpa shida, mwalimu Emilia ndiye aliyeanza kuwagundua,kwa haraka akawafuata.Wakapeana mikono kisha wakafika mpaka ofisini na kuanza mazungumzo.
“Sonia,feel at home”
Mwalimu Emilia,aliyeonekana Mwanamke mtu mzima alimkaribisha Sonia huku akitabasamu.
Kupitia macho na tabasamu la Mwalimu Emilia,Sonia alijifunza kitu,halikuwa tabasamu la kawaida,lilikuwa tabasamu fulani la kimachnoo.
Baada ya siku mbili Dustan akaaga na kuhakikisha kila kitu kilienda sawa kwa Sonia,akamkabidhi pesa za kutosha na kuanza safari ya kurudi zake Tanzania huku nyuma akimuacha Sonia katika maisha mapya.
***
Sonia hakutaka mazoea na mwanafunzi yoyote yule wa chuo,ndiyo ilikuwa tabia yake tangu alipotoka.Wanafunzi wengi walimshobokea kwa nia ya kutaka kumzoea lakini hakuthubutu kujichanganya na wazungu,kila mwanaume alipagawishwa na uzuri wa msichana huyu Sonia.Alikuwa ana mikogo ya kufa mtu!
Ukibahatika kuongea naye basi salamu yake tu.Siku hiyo alitoka darasani akanyoosha moja kwa moja hostel,kutokana na kusoma sana alijihisi uchovu.
Akatembea mpaka chumbani kwake,akavua nguo zake zote mwilini na kuchukua taulo kwa nia ya kwenda kuoga.Katika hali ya kushangaza alikuta mlango wa bafuni umefunguliwa,katika kumbukumbu zake ubongoni hakuacha mlango wa bafuni katika hali aliyoikuta.Akasita kwanza,akatizama huku na kule kisha akaingia na kujifungia kwa ndani.
Akawasha bomba la mvua la maji ya moto,maji yakawa yanatiririka mwilini mwake,akapaka sabuni usoni.Alivyokuwa ameyafumba macho yake, anajisugua akahisi kama kuna mtu nyuma yake.
Hisia zake hazikumdanganya alivyoyafumbua na kupiga jicho mbele ya kioo kilichokuwa mbele yake alimuona mwalimu Emilia yupo nyuma yake,juu hana kitu chochote yaani maziwa yake yapo wazi.
“Shss shss silent please”
Mwalimu Emilia,akamuwekea kidole mdomoni Sonia,huku taratibu mdomo wake ukianza kusogea karibu kabisa na kuanza kumpapasa Sonia!

******
Alikuwa ni mwanafunzi mrefu kiasi mweusi, aliyechanganyika na mataifa mawili,Namibia na Marekani,rangi nyeusi alichukua kwa mama yake na mchanganyiko wa nywele alichukua kote kwa baba na mama yake.
Wazazi wa Sebastian walikuwa wakiishi Marekani na alipelekwa chuo hicho kwa sababu tu,kilikuwa cha Mjomba wake Mr.Spenser Donovan, tajiri aliyetokea kutingisha bara la ulaya na Marekani kwa ujumla, hawakuwa na sababu ya kupoteza ma elfu ya pesa, walimsafirisha mpaka ulaya na kumuanzisha chuo hicho cha Stockholm, nchini sweden.Kutokana na utajiri waliokuwa nao, Sebastian alikuwa ni mwenye dharau,aliringia pesa za baba yake,shida alizisikia tu kwenye historia za kwenye vitabu.Jina lake lilizidi kuwa juu na kupata umaarufu baba yake alivyomtumia pesa za kununulia gari aina ya Lamborghin,akazidi kupeta,mbali na kuwa na dharau Sebastian alijua kwenda na wakati,alikuwa ni chek bobu mkubwa sana,hakuna nguo wala kiatu kilichompita,Jordan,Air max na kila All star itakayotoka ni lazima aiweke mguuni,hiyo ikamfanya azidi kutingisha.Wasichana wengi wa kizungu walijigonga na kumuwinda lakini hawakufanikiwa.
“Who the hell,does he think he is?”(anahisi yeye ni nani?)
“What is wrong Thelma?”(Tatizo nini Thelma)
“That son of a bitch Sebastian,This guy has been blowing up my phone am talking calling me every hour and talking how he wants to hoock up with me,the whole week he has been telling me how special I am and then I decide to give him the time of day and guess what that nigger does!”(Yule mtoto wa malaya Sebastian,huyu jamaa alikuwa akinisumbua ananipigia simu yangu kila masaa,ananieleza atakavyosterehe namimi,kwa wiki nzima alikuwa akinisifia na nikaamua kumpa muda wangu,embu otea alichonifanyia)
“Ooooooohhhhhh!Girllll..what did he doo,tell me,tell me,tell mee...”(Oh niambie niambie,jamaa kakufanya nini,niambie,nambie,nambie)
Carola alitaka kujua ni kitu gani Sebastian alimfanyia rafiki yake kipenzi ambaye kila wakati alikuwa akimuwinda kimapenzi,mbali na hapo kwa asilimia fulani alifanikiwa kumkamata,Thelma alikuwa ni mwanamke wa kizungu,yaani mmarekani, miongoni mwa watu waliokufa na kuoza ni binti huyu aliyekuwa akifanya kazi duka kubwa la nguo.Hakujali kwamba Sebastian ni mwanafunzi wala nini,lakini juhudi zake zilikuwa mbioni kumnasa.
“He rolls up in my house after I had invited him with some random chick and has the nerve to introduce her as his sister and I know this bitch”
Thelma akazidi kumueleza mwenzake jinsi Sebastian alivyoingia nyumbani kwake na msichana mwingine,akazidi kukasirika na kuapia kuwa ni lazima Sebastian angekuwa wake siku moja, mbali na hapo angetumia gharama yoyote ile kumpata.Ukweli ni kwamba Sebastian alikuwa gumzo kwa watoto wa kike.Gari lake lilijulikana kila alipolipaki walijua yupo hapo.
***
Katika hali isiyo ya kawaida baada ya Sebastian kupaki gari yake chuoni aliona kitu kisicho cha kawaida,aligandisha macho yake kwa binti mmoja mweupe aliyekuwa anashusha mabegi yake ndani ya Taxi,alimtizama juu mpaka chini.
“Daaamn!”
Sebastian alisema na kupuuzia, lakini alivyotembea alikuwa akigeuza geuza shingo yake nyuma akimtizama Sonia.
Akamuacha na kuondoka zake.

SIKU zikazidi kwenda mbele,mara nyingi alimuona Sonia kwa mbali,tabia moja iliyomshangaza Sebastian ni kutokushobokewa na binti huyo,ilikuwa ni jambo la ajabu,mgeni yoyote atakayefika chuoni hapo ilikuwa ni lazima ashobokewe, kwa Sonia ilikuwa kinyume kabisa.Hilo ndilo lililomfanya atake kumjua kiundani zaidi.
“Hey baby whatsap”
Hiyo ndiyo salamu aliyotoa Sebastian kwa Sonia,baada ya kuisogelea meza yake.Sonia alimtizama na kumpandisha kutoka chini mpaka juu.
“Am good”
Alitoa jibu huku akisimama na kuondoka zake,jinsi alivyopindisha mdomo wake lilikuwa jibu tosha kuwa hakutaka mazoea,jambo hilo liliwashtua watu wengi kutokana na kila mwanafunzi alimkodolea macho Sebastian.Sonia akaondoka zake huku nyuma akiacha taharuki.

Ukweli ni kwamba Sonia alitingisha chuo kizima kwa uzuri na mikogo,kila mwanaume alimmendea kumpata,wakatumia kila njama na kutuma zawadi kama maua na pesa lakini Sonia hakujibu lolote,aliishia kuvichana na wakati mwingine kukataa kupokea.
Sio kwa wanaume tu peke yao,hata wanawake wenzake walimtamani, sheria ya jinsia moja katika nchi hiyo ilihalalishwa,yaani swala la ushoga na usagaji lilikuwa la kawaida sana,Kitendo cha Mwalimu Emilia kumuona Sonia alimtamani na aliapia ipo siku angekuwa mke wake,kwa wiki nzima alijaribu kufanya upelelezi na kugundua hostel anayoishi,akatoka ofisini kwake moja kwa moja na kunyoosha mpaka anapolala Emilia akafungua mlango wa bafuni na kujificha nyuma ya kipazia huku akimsubiri Sonia kwa kihoro,
alijipanga kumfanyia vitu hadimu.Mwalimu Emilia alijiona kama ni mwanaume, kitaalamu watu hawa huitwa, Lesbian.
Kitendo cha Sonia kuvua nguo zake baada ya kuingia bafuni, nayeye alichojoa yake ya juu na kuanza kumpapasa Sonia.
“Hey”
Sonia alikema kwa hasira na kumsukuma Mwalimu Emilia.
“Tulia,usipige kelele”
“Unataka nini mwalimu?”
“Penzi”
“Niniii?,mbona sikuelewi naomba uniache”
“Siwezi kukuacha”
“Haiwezekani,mimi nakupenda”
“Unasema nini wewe?”
“Ndi....”
Kabla ya kumalizia sentensi yake,sauti nzito ilisikika kutokea mlangoni, Sonia ndiye alikuwa akiitwa na mlango ulisikika ukifunguliwa.
“Sonia,are you there?”
NI sauti ya Sebastian ndiye iliyokuwa inasikika,alikuwa teyari amefika ndani na mzigo mkubwa wa maua mkononi,alikuwa amenyuka vibaya sana, yaani alivunja kabati kama waswahili wanavyosema.
Sonia akapata upenyo akatoka na kanga moja mwilini akamkimbilia Sebastian na kusogea karibu.
“Bro...”
Sonia aliongea kwa hofu akiwa mikononi mwa Sebastian,kitendo cha mwalimu Emilia kutokeza nje kilimshangaza lakini alianza kuelewa nini kilichokuwa kinaendelea.Wasiwasi wake ulikuwa kwa Sonia, alidhani wenda ni msagaji na ndiyo maana alikuwa hapendi wanaume na kutokana na tetesi alizowahi kusikia juu ya mwalimu Emilia,ilimfanya aamini picha aliyoiona.
“Sebastian,simwelewi mwalimu Emilia”
“Kafanya nini?”
“Hata sijui nikwambie nini..lakini alitaka kunifanyia vitu visivyo staili”
“Usijali Sonia,vaa nguo tuondoke”
Hakuwa na chaguo lingine zaidi ya kubeba nguo zilizokuwa tayari zipo kitandani na kuzama bafuni,alivyotoka alikuwa teyari keshavaa.
Wakatoka na Sebastian na kumuacha mwalimu Emilia chumbani.Wakaenda moja kwa moja mpaka ndani ya Ramborghin ya Sebastian na kuondoka zao,ilikuwa ni jioni ya saa kumi.
Wakanyoosha mpaka Tcentralen katikati ya jiji katika mgawaha mmoja wa Mackdonald,wakaingia na kutafuta sehemu ya kukaa.
“Vipi,agiza Burger ule”
Sebastian alisema.
“Ahsante,nimeshiba”
“Hapana usinifanyie ivyo,basi hata juisi”
“Sawa”
Sonia na Sebastian walianza mazungumzo yao wakitumia lugha ya kiingereza.
Sebastian alitaka kujua zaidi kuhusu maisha ya Sonia,akaanza kumchimba.Bila hiyana Sonia akaanza kufunguka moja baada ya jingine.
“Ndio,kwa mama yangu nipo mmoja kwa baba tupo wawili”
Hivyo ndivyo,Sonia alivyokuwa akijua.
“Wewe je?niambie kidogo kuhusu wewe”
Sonia nayeye akataka kumjua Kiundani.
“Mimi ni mtoto wa kwanza na wa mwisho,Baba yangu Mtu wa Marekani Mama yangu ni raia wa Namibia,wote wanaishi Marekani....”
Sebastian alisema kila kitu kuhusu yeye kwa ufupi wakiendelea kula na kunywa.
Kila mtu akamfurahia mwenzake,wakahama kiwanja na kuingia kungst'agorden katikati ya jiji,wakazama mpaka mgawaha ulioitwa 'Friday' wa kitasha,watu wa hali ya chini hata siku moja hawakuweza kuthubutu kupitisha pua zao,na tangu mgahawa huo ufunguliwe Sebastian mwenye rangi ya kiafrika ndiye alikuwa wa kwanza kufanya matanuzi,
alizoeleka kiasi kwamba hata wahudumu walimfahamu.
“Sebastian,What do you prefer today?”
Muhudumu alimuuliza.
“As usually”(Kama kawaida)
“And you?”
Lilikuwa ni swali lililomlenga Sonia,hakuwa na jibu la moja kwa moja akamtizama Sebastian.
“Bring her,chips chicken”
Sebastian akajibu,Muhudumu akaandika kwenye kimashine maalumu akitoa oda jikoni kisha kuondoka zake,Chakula kikaletwa wakala na kunywa.
“Sonia”
Sebastian akaita huku akimtizama Sonia machoni.
“Abee”
“Wewe ni mzuri sana”
“Ahsante”
“Bado sitaki kuamini kuwa Tanzania kuna warembo kiasi hiki,bado sitaki kuamini kwa kweli”
“Amini ivyo,mimi ni mtanzania halisi kabisa”
Sebastian akazidi kumimina sifa kemkem,mbali na hayo moyo wake ulimsukuma awe naye kimapenzi,hilo hakutaka kuliweka ndani ya mtima wake.
“Naomba tukitoka hapa,twende sehemu nzuri sana nikupeleke ukafurahi”
“Hapana nimechoka,nitarudi tu kulala,lakini namuhofia yule mwalimu”
“Mwalimu yupi?”
“Emilia”
“Alafu hujaniambia ilikuwaje”
Sonia akaeleza kila kitu.
“Wazoee,ndiyo ilivyo huku watu wa jinsia moja wanasheria zao na pia vilevile una uhuru wa kuwakataa ivy......”
“Baby,Darling I miss you,where have you been my love?”(Mpenzi nakumisi ulikuwa wapi)
Ilikuwa ni sauti iliyomchangaya akili Sebastian,akamgeukia Thelma, kabla ya kuamua chochote lips zake zilikuwa zimemezwa na mzungu huyu aliyekuwa kafa kaoza kwa Sebastian.


*****
Hakuna kitu kilichomuharibia pozi kama Thelma kumpiga denda mbele ya Sonia,alivyotaka kumsukuma alikuwa teyari amechelewa na yupo mdomoni mwake,kilikuwa ni kitendo cha ghafla yaani cha kufumba na kufumbua na ndiyo maana Thelma alifanikiwa.
“Nakumisi sana Sebastian wangu,ulikuwa wapi? juzi nilipata simu yako lakini sikuwa nchini nilikuwa Italy,vipi zawadi zangu ulipata?”
“Thelma unajua kuwa nina kuheshimu sana,kwanini unanibusu busu bila ridhaa yangu?”
“Lakini mpe..”
“Lakini nini?Lakini nini?sitaki na sipendi mimi nawewe kwanza naomba utambue ni marafiki tu yaani washkaji wa kawaida wa kupeana salamu basi,kitu ulichokifanya umevuka mipaka,kwanza nani kakuita hapa?”
“Sebastian...”
“Nani kakuita hapa?Naomba uwende tuna mazungumzo”
“Mazungumzo gani ambayo mimi siruhusiwi kuyasikia?”
Thelma akaweka ngumu,mazungumzo yalifanyika kwa lugha ya kiingereza na yote hayo Sonia aliyasikia lakini alizuga na simu akijifanya anachati.
“Sawa,wewe baki...Sonia embu tuhame hapa”
Hivyo ndivyo ilivyokuwa,Sebastian akamkamata mkono Sonia na kutoka zao nje wakamuacha Thelma amebenua mdomo,kitendo hicho kilimkasirisha kwa kiasi cha kutosha.

Mkono kwa mkono Sebastian na Sonia wakaongozana mpaka ndani ya gari.
“Wapi sasa tunaenda?”
“Kiwanja kingine”
“Hapana Sebastian,nahitaji kupumzika kesho nina shule mwenzio”
“Kweli?”
“Ndio”
Sebastian alikuwa ni mwanaume mwelewa,akakubaliana na matakwa ya Sonia,akawasha gari wakanyoosha mpaka katikati ya mji,gari la Sebastian likapaki nje ya hostel za wasichana Sonia akashuka,wakatakiana usiku mwema.
“Hey Sonia”
Sebastian aliita kwa sauti, alionekana ni kama mtu aliyesahau kuongea kitu.Sonia akageuka lakini hakutaka kurudi nyuma,hiyo ilimaanisha Sebastian ndiyo amfuate,kitendo hicho kikafanyika,Sebastian akatembea kwa mikogo mpaka karibu na Sonia.
“Kuna kitu ulisahau kunipa”
“Kitu gani?”
“Namba zako za simu”
“Alafu kweli”
Hapohapo wakabadilishana namba za simu.
Kauli yake ambayo alisema kwamba hakuna mwanamke wa kiafrika ambaye ataizuzua akili yake sasa aliipuuzia,ukweli ni kwamba katika maisha yake hakutaka kuchafua rungu lake kutembea na msichana wa kiafrika,Sebastian alikuwa na mahusiano ama marafiki wa kike wa kizungu peke yake,Mpenzi wake wa mwisho alikuwa Mmarekani,huyu waliachana miezi mitatu nyuma,na hakutaka kabisa kuweka mazoea naye hata kidogo.
Sura ya Sonia ilikuwa ikimtesa kichwani mwake na aliamini huyo ndiye angekuwa mwanamke wake endapo angekubali swala hilo.
Hakutaka kuidhulumu nafsi yake,Kila kukicha akawa hakauki hostel kwa Sonia,swala la kumtoa chuoni mpaka anapolala akalichukua yeye,baadhi ya watu walidhani ni ndugu sababu ya rangi ya ngozi zao.Lakini ukweli ulibaki kwamba Sebastian anampenda Sonia.
“Leo twende wapi Sonia?”
“Kuna sehemu niliipenda,juzi pale kwenye mchezo wa balling sijui panaitwaje”
“Basi badili nguo twende”
Ndani ya mwezi mmoja wakawa wameshibana kila mtu alimzoea mwenzake,haikuweza kupita siku bila ya mmoja kumuona mwenzake,hapo ndipo Sebastian alipoanza kutupa mawe na kuelezea jinsi anavyohisi ndani ya moyo wake,maneno hayo alimwambia wakiwa sehemu moja iliyotulia sana tena usiku hakuna kelele.Katika kuongea kwake Sebastian hakuacha kumwambia kuwa yeye ni mzuri.
“Hapana Sebastian,sisi ni kama ndugu sasa hivi..kwahiyo hilo swala lifute akilini”
Hilo ndilo jibu alilotoa Sonia.
“Usiseme hivyo Sonia,unakuwa unakosea sidhani kama unakuwa sahihi ukisema sisi ni kama ndugu,ni kwasababu ya rangi?”
“Sina maana hiyo,nina maana kwamba wewe ni kama kaka yangu,kwahiyo swala la mapenzi tukianzisha litakuwa gumu kidogo,jinsi nilivyokuzoea tukiwa wapenzi ninajua mambo mengine hayatoenda sawa,ngoja nikupe mfano”
“Enhee”
“Kwenye mapenzi kuna mambo mengi ujue,kuna kugombana unadhani mahusiano yetu yatakuwa kama haya tuliyonayo,fikiria hilo Sebastian”
“Mimi nishafikiria kabla hujaniambia na ninapenda kukuhakikishia kwamba uhusiano wetu tulionao utazidi na utadumu zaidi na zaidi”
“Wanaume mna maneno matamu sana,hivi unajua kuwa hayo maneno siyo mageni kwangu,hakuna neno jipya hapo,nikuulize swali?”
“Niulize”
“Mfano,nikikataa kuwa na mahusiano nawewe kama unavyotaka,nikakataa katakata kuwa nawewe,utachukuwa hatua gani?utatafuta mwanamke mwingine au?”
“Mhh aaah....hapo itategemea,unajua mapenzi sio kitu cha kulazimishana,moyo utaniuma lakini nitavumilia itanichukua muda mrefu kutafuta msichana mwingine sitaki kukudanganya kwamba sitopenda tena,huo utakuwa ni uwongo mkubwa.Mimi ni mwanaume mkweli.....”
Mbali na maswali karibia laki moja aliyouliza Sonia lakini aliendelea kusimamia msimamo wake kwamba HAKUWA TAYARI kuwa kimapenzi na Sebastian,hilo ndilo lilikuwa jibu lake na akahitimisha kuwa anahitaji kwenda kupumzika kichwa kinamuuma.
“Nikutafutie dawa?”
“Hapana,nipeleke tu hostel nikalale”
****
Sebastian bado hakukata tamaa ya kumtaka Sonia kimapenzi,ndiyo kwanza aliongeza kasi ilikuwa kila akimuona Sonia amesimama na Mwanaume wivu unamkaba,hakutaka kuona swala hilo mbele ya macho yake.
“Stay away from her,understood?”(Kaa mbali nayeye,umenielewa)
Hiyo ndiyo kauli aliyotoa Sebastian baada ya kuona mwanafunzi huyo wa kiume alikuwa anaongea na Sonia muda mfupi uliopita.
“Meeeen,what is wrong with yaaah?who the hell are you?get lost m....”
Kijana wa kizungu akajibu kwa nyodo huku akirusha rusha mikono yake kama mwanamuziki wa 'hiphop'.
“Puuuuuu”
Kilikuwa ni kishindo cha ngumi,Sebastian alimkatisha sentensi yake kwa kumpiga ngumi ya mdomo.
“Fuc*** you,i said Fuc*** you”
Hapo ndipo ugomvi ulipoanzia,ikawa rusha ngumi nijibu.Wanafunzi wakaacha kusoma madarasani wakaenda kuwa achanisha.
“Leave me Dominic lemi teach this Motherfuck**”
Sebastian alitaka kujitoa mkononi mwa rafiki zake,alikuwa amepandwa tayari na hasira iliyochanganyika na wivu.
Na hiyo ndiyo ilikuwa sifa yake,alikuwa ni mwenye hasira za karibu.Kutupa ngumi ilikuwa ni jambo la kawaida,wanaume wengi wa kizungu walimuogopa na walijitenga naye walinimuelewa jinsi gani alivyokuwa mkorofi hasa akijibiwa vibaya.
Haraka akapelekwa ofisini ili kujibu mashtaka.
“Sebastian mara ngapi lakini unakuwa unarudia kosa lile lile?au kisa hiki chuo cha mjomba wako?”
“Hapana mwalimu bahati mbaya”
“Bahati mbaya nini?kila siku unakuwa mkorofi tu,jina lako naliweka kwenye blacklist,tuone jeuri yako itaishia wapi?”
“Usifanye ivyo tafadhali”
“Wacha nifanye hivyo maana husikii,nikiweka jina lako kwenye blacklist ndiyo utajua huko mbele ya safari,tuone utaishia wapi,embu potea ofisini kwangu”
Swala la kuingizwa 'blacklist' na jina lake kuingizwa kwenye system kwamba alikuwa ni muhuni na mtovu wa nidhamu kulimaanisha kuwa cheti chake kitachafuliwa na asingeweza kufanya jambo lolote lile, hilo hakulijali sana,ni bora ampate Sonia lakini jina lake lewekwe popote pale,aliamini kwamba Sonia ndiye kitu muhimu katika maisha yake.

Hakufanya kitu kingine,baada ya kutoka ofisini kwa mwalimu, akanyoosha mpaka ndani ya gari lake na kulitoa kasi mpaka sehemu aliyopanga yaani geto,akafika na kujitupa kitandani.
Alivyoshtuka ilikuwa tayari saa mbili za usiku,akachukua simu mezani na kukuta missed call nane,zote zilitoka kwa Sonia.Hapohapo bila kupoteza wakati akampigia.
“Sonia,mambo vipi?”
“Safi,upo wapi?”
“Nipo kwangu”
“Nimesikia leo umepigana,nini kilitokea?”
“Nitakuja kukwambia, upo wapi kwani?”
“Hostel”
“Nakuja sasa hivi”
Sebastian akasimama,akavua shati na kuingia mpaka bafuni,akautizama mwili wake ulivyochafuka alama za 'Tatoo',mwili wake haukutofautishwa na gazeti,alikuwa amejichorachora kifuani maandishi,yakapita mpaka tumboni,Mgongoni ndio usiseme,haikuwa rahisi kwa mtu kugundua kama ana michoro yoyote ile kama akiwa amevaa shati.
“Itabidi moja niandike jina la Sonia,wapi sijui niliandike”
Sebastian,alijiuliza huku akijitizama kama kuna nafasi ya kuchora tatoo nyingine,akajicheki vizuri.
“Nitachora shingoni,ili aione iwe rahisi,tena leoleo”
Alivyomaliza kuoga,akaingia kabatini na kutinga pamba safi,akaingia kwenye kabati lingine la viatu lililokuwa na pair sabini,akachuka Air max na kuiweka pembeni.Akatafuta t.-shirt na kuiweka mwilini.Akavaa kila kitu.
“Sonia,nitachelewa kidogo napeleka gari Gereji”
Sebastian alipiga simu na kumdanganya Sonia.
“Poa,ukiwa unakuja utaniambia”
“Ok”
NUSU saa nzima akaendesha gari mpaka alipofika sehemu moja ya watu wenye ngozi nyeusi, yaani black America.Mtaa unaochora watu tatoo.
“Yoooh bob tsup nigger, i need a tatoo,come I show you”
Sebastian akamuita mmoja wa wataalamu akampa maelekezo,jinsi ya kufanya.
Wino ukapakwa na mashine ikaletwa, Sebastian akaanza kuchorwa.
Ndani ya dakika ishirini kila kitu kilikuwa shwari.NO MATTER WHAT, I WILL LOVE YOU FOREVER SONIA,hayo ndiyo maandishi yaliyosomeka shingoni mwa Sebastian na yalionekana kabisa.Akafurahi na kulipa kisha kuondoka zake,hakujali hata kama angekataliwa lakini tatoo hiyo ingempa kumbukumbu kuwa kuna msichana alimpenda.Kitu cha kwanza baada ya kufika alimuomba Sonia watoke kwani anataka kumpeleka sehemu nzuri.
Sonia akavaa harakaharaka wakaingia ndani ya gari.
“Mhhh”
Sonia aliguna akiwa ndani ya gari huku akiitizama shingo ya Sebastian.
Sebastian alishaelewa tayari ujumbe wake umefika, lakini akajifanya hana habari yupo juu ya usukani,anatingisha kichwa na kuongeza sauti ya redio na mziki wa Busta Rhymes ft Mariah Carey ulioitwa, 'I know what you want'.Ndiyo uliokuwa ukidunda,akawa anatingisha kichwa chake huku akifatisha maneno ya nyimbo.
“BABY IF YOU GIVE IT TO ME,I WILL GIVE IT TO YOU,I KNOW WHAT YOU WANT”
Sebastian akafatisha,jinsi mwimbo unavyokwenda.Sonia akapunguza sauti.
“Sebastian,Sebastian...”
“Naaam”
“Hiyo tatoo umechora lini?”
“Ipi hiyo?”
“Embu toka hapa usijifanye hujui,hiyo hapo shingoni,embu sogea karibu”
Sebastian akasogeza shingo yake karibu kabisa na Sonia ili ichunguzwe,kama umeme Sebastian akageuza mdomo wake akamvuta shingo Sonia,hapohapo akaanza kumnyonya mdomo.
Ilikuwa ndiyo mara ya kwanza kupigwa denda katika maisha yake,akahisi kama amepigwa na shoti ya umeme,damu yake ilimuenda mbio, nguvu zikamuishia kabisa!.


*****

Sio kwamba alishindwa kujipachua mikononi mwa Sebastian la hasha!nguvu zilimwishia akashindwa kufanya hivyo,akahisi kama siyo yeye fikra zake zikasafiri maili mia moja,vitu kama vijidudu vikawa vinapita ndani ya mwili wake.Bado alikuwa midomoni mwa Sebastian wanapigana denda huku akiwa ameyafumba macho yake anahema ndani kwa ndani.
“Wiu wiu wiuu”
Kilichomshtua Sebastian ni kelele za king”ora cha gari la polisi,kitendo cha kuangalia mbele na kumuachia Sonia,akagundua kwamba yupo pembeni ya barabara amehama njia,ilikuwa ni kosa kubwa sana na polisi wa nchi hiyo muda wote walikuwa wakizunguka zunguka ili kuangalia usalama.
Akasimamishwa na kupaki gari pembeni,gari la polisi likapaki nyuma yake kama mita saba,askari wa kizungu akashuka huku akiwa ameshika kiuno chake kakamata bastola yake ili kujihami.Akasogea mpaka kwenye gari la Sebastian.
“Habari yako kijana?”
“Salama afande,za kazi?”
“Nzuri,mbona unayumba barabarani,naomba leseni yako tafadhali”
Hakukuwa na namna ya kufanya Sebastian akatoa leseni na kumkabidhi polisi wa usalama barabarani.
“Mr.Sebastian,nini kilichokuwa kinakufanya uyumbe barabarani?umelewa au?”
“Hapana afande”
Sebastian alijaribu kumtia sound na kumuimbisha polisi akijaribu kumpa chochote kama kifuta jasho, lakini alikataliwa,leseni yake ikachukuliwa na alitakiwa kuifata kituo cha polisi akiambatanisha na barua ya kosa alilofanya pamoja na faini ya dolla elfu moja,hivyo ndivyo ilivyokuwa.

Hapo aliachiwa lakini bila leseni yake,akakosa raha.Akaendesha gari mpaka kwenye moja ya gorofa kubwa na kushuka,akazunguka upande wa pili na kumfungulia mlango Sonia.
“Shuka malkia wangu”
Sonia akashuka wakaongozana mpaka kwenye moja ya mgawaha na kuketi,huku wakianza kupiga stori mbili tatu.
“Sebastian,upo sawa?”
“Nipo sawa,nipo sawa kabisa,kunywa kinywaji chako”
“Pole na kilichokukuta”
“Ahsante usijali”
“Enhee nilitaka kusahau,kwanza kwanini ulipigana? alafu hapo shingoni sijaelewa vizuri”
Sebastian akamtizama vizuri Sonia machoni,akaiangalia midomo ya mrembo huyo ilivyokuwa laini kama imepakwa grisi,kitendo kilichotokea ndani ya gari dakika chache zilizopita kilimkosha, bado hakuamini kama alikuwa tayari kamla denda Sonia,ndani ya moyo wake akajiona kama ni mshindi,akajipa matumaini kwa hatua aliyofikia.
“Kuna bishoo mmoja alitaka kuniletea za kuleta akawa anachonga chonga,nikamfunza adabu kidogo...nikamweka kwenye mstari”
“Ukorofi sio mzuri Sebastian,mimi sipendi mtu mkorofi.Kwahiyo ipo siku hata mimi utanipiga?”
“Naanzaje kukupiga sasa?”
“Si nikikukera”
“Siwezi kufanya hivyo”
“Na hiyo hapo shingoni?”
“Nini?”
“Sebastian,usijifanye hujui,mwone vile...hiyo tatooo..Embu niambie kuhusu huyo msichana uliyemwandika hapo”
Huo ndiyo ukawa muda muafaka,Sebastian akachukua nafasi hiyo kwa utulivu kabisa akaanza kumtongoza Sonia upya,akamwambia ni jinsi gani moyo wake ulivyokuwa unamuuma.

Akaongea kwa simanzi na kutumia swaga zote anazozijua,Sebastian alikuwa ni mjanja wa maneno.Alikuwa akijibu maswali ya Sonia kwa umakini sana bila kujikanyaga.Katika kila alilosema hakuacha kusema neno NAKUPENDA SONIA WEWE NI MZURI neno hilo alilirudia sio chini ya mara kumi na saba.
“Hapana Sebastian,bado sikuamini.Moyo wangu unasita sana”
Bado Sonia aliweka ngumu,ni kweli moyo wake ulikuwa mzito lakini hakuelewa kama ni uwoga au wasiwasi.Vitu hivyo alishindwa kuvichanganua sababu alikuwa bado ni mgeni wa mapenzi.
“Kwani Sonia ulishawahi kuwa na mwanaume?”
“Ndio,nilikuwa nao wengi sana,hatimaye walinichezea na kuniacha.Sina hamu nao tena”
Sonia alidanganya.Ili tu ajenge hoja ya kumchomolea Sebastian.
“Hao ni wanaume wengine,sio Mimi.Mimi ni tofauti na ndiyo maana hata vidole vyetu havilingani hata siku moja,kuna kirefu,kifupi chembamba na kadhalika”
“Nikwambie kitu Sebastian”
“Niambie ndio”
“Hayo maneno unayoniambia,sio mageni kwangu yote nilishaambiwa sana,nikapewa na mifano milioni kidogo”
Sebastian akapata na kigugumizi akashindwa ni kwa namna gani aingize gia nyingine.
***
WALA HAKUKATA tamaa,aliendelea kuwa karibu sana na Sonia yaani bega kwa bega,walikula wote,walisoma pamoja,waletembea wawili,kifupi walishirikiana kwa kila jambo.
Siku moja Sonia alishindwa kuelewa ni kitu gani kilimpata Sebastian, sababu hakupigiwa simu na wala hakumuona chuoni,jambo hilo halikuwa la kawaida hata kidogo,alivyoamua kumtafuta hewani pia hakupatikana.Kifupi alimzoea sana na hakuweza kupitisha hata masaa bila ya kumuona,walikuwa kama mapacha.
“Huyu atakuwa amepatwa na nini?”
Sonia akajiuliza maswali,baada ya kufika hostel.Akajitupa kitandani na kujaribu kupiga simu ya Sebastian lakini swala lilikuwa lilelile Sebastian hakupatikana hewani.
“Ningeenda kwake lakini sipajui,subiri nimtafute Alhadro labda ataweza kunielekeza”
Hapohapo Sonia,akaangalia namba ya mwanafunzi mwengine ambaye huwa wapo kundi moja la 'discusion' na kumpigia simu na kumuulizia.
“Una paulizia kwa Sebastian?”
“Ndio”
“Wewe upo wapi?”
“Nipo Hostel”
“Sawa,nakuja kukuchukua nikupeleke kwake”
“Ahsante sana”
Simu ikakatwa.
**
Ilikuwa ni kama Ahsante Mungu kwa Alhandro,katika wanafunzi ambao waliokuwa wanammezea mate Sonia Alhandro alikuwa mmoja wapo,lakini alikuwa domo zege siku zote.Hakupata nafasi hata moja ya kuzungumza na Sonia,alikuwa ni mwanaume wa kizungu kabisa na alivutiwa na msichana huyu wa kiafrika,kitendo cha kuweka ukaribu na Sebastian kilimuuma roho kupita kiasi,alichofanya ni kutafuta simu na kumpigia rafiki yake Linus na kumueleza kwamba anahitaji geto.
“Poa poa mimi sipo,funguo zipo juu ya mlango”
“Sawa”
Alivyomaliza kuongea na simu akavaa harakaharaka,kutokana na alikuwa ana mashine ya kuprint picha akaingia kwenye mtandao harakaharaka na kuiprint picha ya Sebastian.

Baada ya dakika kadhaa akatoka nayo.Haraka akapanda treni mpaka anapoishi rafiki yake Linus,akachukua funguo juu ya mlango akafungua na kuingia,akabandika picha za Sebastian ukutani.Na kuweka kila kitu sawa kabisa, chumba kikaonekana ni cha Sebastian,hakukaa hata dakika moja simu ya Sonia ikaita.
“Nipo njiani,nakuja kukuchukua,nisubiri nje hapo Hostel”
“Mimi nishajiandaa tayari,jamani”
“Sawa nakuja”
Alhandro akatoka chapchap,akaondoka akapanda treni.Kivyovyote alijiapia kwamba ni lazima amvue Sonia nguo yake ya ndani hata kama kwa kumbaka.Dakika kumi alikuwa tayari amefika hostel akaonana na Sonia.
“Samahani kwa kukuweka”
“Usijali,vipi tunaenda sasa hivi?”
“Ndiyo,tunaenda sasa hivi nilikuwa naye muda mfupi tu kwake”
Alhandro akadanganya.
“Basi nipeleke jamani,mbona ananifanyia ivyo.Alikwambia chochote kuhusu mimi?hajakwambia kwamba nilimuudhi?”
“Wala,hajaniambia”
“Okay twende”
Wakatembea wote huku Sonia akiwa mwenye furaha lakini moyoni alipanga kuongea mengi na Sebastian,alihisi kuna kitu kisichokuwa cha kawaida.Wakaingia ndani ya treni ya umeme,mwendo wa dakika chache walikuwa teyari wanashuka.Wakatembea hatua chache mpaka mlangoni.
“Sebastian,Sebastiiian”
Alhandro ndiye alikuwa akijifanya kuita,ilikuwa ni zuga tu,ukweli ni kwamba hakukuwa na mtu ndani ya nyumba hiyo.
“Atakuwa ametoka mara moja”
Alhadro akatoa funguo mfukoni na kufungua mlango.Cha kwanza kuonekana ni Picha ya Sebastian ukutani,Sonia akajisikia amani ya moyo,muda wote alikuwa akitaka kuonana na Sebabstian,jinsi alivyo mmisi hakuelewa akimuona angefanya kitu gani.
Huku na kule Alhandro akaingia kwenye friji na kutoa kinywaji akamkabidhi Sonia ili anywe.
“Subiri hapo ili nimuulize yupo wapi”
Alhandro akajifanya kuigiza kuongea na Sebastian kwenye simu.Alivyokata alifunga mlango na funguo bila ya Sonia kujua.
“Mbona hunywi kinywaji?”
“Hapana,sijisikii kunywa chochote kwa sasa hivi”
Sonia hakusikia amani yoyote ile aliamini angepata amani endapo angemtia machoni Sebastian.
Kitu kilichomshangaza ni kumuona Alhandro anavua shati lake tena mbele yake,mara ghafla akamsogelea na kuanza kumshika mashavu.
“Vipi mwenzangu?”
Sonia akauliza.
“Vipi nini?”
Kwa nguvu Alhandro,akaanza kumvuta kitandani huku akimkamata kiuno hapo ndipo somo lilipobadilika.
“Griii griii griii griiii”
Simu ya Sonia iliyokuwa mfukoni ilianza kuita,akamsukumiza Alhandro pembeni na kuitoa,jina lililokuja juu ya kioo ni SEBASTIAN kabla ya kuipokea,Alhandro akamvaa simu ikadondoka.
Ukweli ni kwamba alishaelewa kuwa alihitajika kubakwa na alitaka kujitetea kwa namna moja au nyingine.
Kuipokea simu ya Sebastian ndiyo ingekuwa ponea yake.
Alhandro alikuwa teyari kachemka, asingeweza kumuacha Sonia hivi hivi, akaikamata nguo yake ya juu,akaichana kama karatasi la gazeti.
Sonia akabakiwa na sidiria peke yake,alikuwa teyari yupo kitandani anajaribu kupambana na mmbakaji,hapo ndipo alipotulizwa na ngumi ya mdomo na damu zikaanza kumvuja.
Akawa hana nguvu tena analia na kupiga kelele,akapapasa papasa mkono na kugundua kuwa ameshika simu yake,alivyotaka kuipokea ikakata.
Akawa amekata tamaa tayari,miguu yake ikapanuliwa sketi yake ikateremshwa,akabana miguu yake kwa nguvu.Akapigwa ngumi nyingine mdomoni iliyomfanya atoke damu nyingi sana,zikachafua mpaka shuka.
“Griii griiiii griiii”
Simu ikaanza kuita mfululizo,Sonia akajikakamua akakamata vizuri na kuipokea lakini alishindwa kuiweka sikioni.
“Halloo halloooo”
Upande wa pili wa simu ndiyo ulikuwa ukisikika.Sonia bado aliendelea kulalamika akiomba msaada.
***
Simu yake haikupatikana tangia asubuhi kwasababu aliizima ili aiwashe asubuhi ya kesho yake,baada ya kuamka tu,kwa bahati mbaya aliisahau chumbani kwake na kwenda kituo cha polisi ili kuikomboa leseni yake ya udereva na kulipa faini kwa kosa alilolifanya.
Ni wazi kwamba alimmisi Sonia kupita maelezo yaliyojitosheleza.Kwa masaa mengi alikuwa kituo cha polisi anaandika maelezo na kufatisha taratibu zingine za kisheria.
Alivyorudi jioni alikuwa amechoka na cha kwanza kukifanya ni kumtafuta Sonia hewani,ili wakutane waongee.Simu yake iliita bila kupokelewa.
“Au atakuwa kanuna?Tafadhali Sonia usinifanyie hivyo”
Sebastian aliendelea kuongea mwenyewe maneno hayo huku simu ikiendelea kuita,ikakatika.
Akapiga kwa mara nyingine,simu ilivyopokelewa alishtuka kusikia kelele za Sonia akiomba msaada,akashindwa kuelewa ni kitu gani akifanye.
“Halloo Halloo Soniaaaa,Soniaaaaaa,Soniaaaaa”
Sebastian akaita bila mafanikio,akili iliyomjia harakaharaka ni 'GPRS track' ya simu.'Google map',simu ikampa Adress, ulikuwa ni mwendo wa lisaa limoja kwa gari mpaka kufika alipo Sonia anaomba msaada lakini kwa treni ni dakika kumi.
Ilikuwa ni lazima awahi na atumie treni ya umeme,
haraka akachomoka kama mkuki na kuvaa koti la baridi,akakimbia na kupiga watu vikumbo,kwenye ngazi za umeme yeye hakuwa na haja ya kusimama ili zimpandishe akakimbia,mpaka juu kabisa akazama kwenye treni.
Dakika kumi baadaye akawa amefika tayari kwenye nyumba ambayo simu yake imemuonesha.
Akafatisha simu mpaka kwenye chumba,Akatingisha mlango lakini haukufunguka.Akarudi nyuma na kuupiga teke kwa nguvu,mzima mzima akaingia nao.
Alichokiona hakukiamini,
“What the fuc***”Alikema.
Machozi ya hasira yalimtoka,alimuona Alhandro yupo juu ya Sonia ndiyo anamvua chupi.
Damu zilikuwa zimetapakaa juu ya shuka na jinsi Sonia alivyokuwa akivuja damu,ndiyo ikamtia hasira zaidi akavimba kama chura.
Akatembea na kuitupa meza pembeni, akamvuta Alhandro akachukua kichwa chake na kukibamiza ukutani.Kwa hasira alizokuwa nazo hiyo haikutosha, akazidi kumfuata,ili kuendeleza kutoa kipigo.


******

Hakuna siku aliyokuwa na hasira kama siku hiyo katika maisha yake,siku yake iliyokuwa na furaha ikaharibika mara moja.Kitu kama kiungulia cha moto kilimkaba kohoni,akashindwa hata kuhema vizuri hiyo yote ilikuwa ni hasira iliyokidhiri.
Alimvuta Alhandro na kumtandika ngumi ya mbavu akamsogeza na kumpiga kichwa puani,kitendo cha kugeuza shingo yake na kumuona Sonia ametulia damu zinamvuja kikamzidisha hasira,lakini kuna kitu ndani ya moyo wake kikamwambia 'STOP' amuwahishe Sonia Hospitali kwanza,kama swala akaruka kitandani na kushika kifua cha Sonia,akazidi kuingiwa na wasiwasi sababu hakusikia mapigo yake ya moyo yakidunda.

Akaweka sikio lale kifuani lakini hali ilikuwa hivyo hivyo,alichofanya ni kujaribu kumpa huduma ya kwanza,akainama kidogo na kuanza kumpulizia pumzi kupitia mdomoni.
“Sonia..Soni.a come on wake up”
Akazidi kutoa huduma ya kwanza,lakini hali ilikuwa ivyo ivyo.Haraka akamfunika na shuka na kumuweka mikononi mwake,akaanza kutoka naye nje.
“Help...Heeeeeelp,Heeeeelp”
Sebastian aliomba msaada wa haraka huku akitoka nje akatokeza barabarani,kila mtu aliyemuona alimpita,bahati nzuri taxi moja wapo ilikuwa inashusha abiria,haraka akakimbia na kujichomeka ndani.Hali hiyo ilimshtua sana dereva.
“Any near hospital please”
“Okay sir”
Gari likatimka,Moja kwa moja mpaka hospitali,alivyofikishwa akawekwa juu ya machela.Madaktari wakaanza kumshambulia,wakamtundikia dripu huku wakijaribu kumwangalia kwa kina mgonjwa wao.
Wakamuingiza ndani ya chumba maalumu kwa ajili ya kumuangalia.Sebastian akabaki nje kwenye kioo kikubwa akitizama kila madaktari walichokuwa wakimfanyia Sonia,Mara ghafla madaktari walianza kuangaliana na kutingisha vichwa vyao,picha iliyomjia kichwani haikuwa nzuri, kulikuwa kuna kila dalili kwamba kuna habari mbaya.Moyo wa Sebastian ukazidi kudunda kwa kasi,akazidi kuingiwa na hofu hasa madaktari walipoanza kupiga piga kifua cha Sonia,akazidi kupagawa.
***
Madaktari ndani ya wodi walizidi kuchanganyikiwa lakini hawakutaka kuchafua CV zao,ilikuwa ni aibu kubwa kwa madaktari wa kizungu mgonjwa kufia mikononi mwao,kutokana na hali aliyokuwa nayo Sonia,ulihitajika uangalifu wa juu, hivyo ndivyo walivyofanya madaktari saba waliokuwa wanamshughulikia.Mapigo yake ya moyo yalikuwa chini na walibidi wayashtue,wakaanza kumpiga piga kifuani na kumchoma sindano .
“Bring Saditerim 12Miligram now,she is loosing”
Dokta Filip aliongea kwa kufoka,jambo hilo likafanyika mara moja.Mkono wa Sonia ukavutwa akadungwa sindano ya dawa.Ndani ya dakika moja mapigo yake ya moyo yakakaa sawa,hapo ndipo Dokta Filip alipoonesha tabasamnu,kwake ikawa kama ushindi.Akaweka kila kitu sawa.Akatoka nje huku akiwaachia madaktari wenzake ujumbe kuwa wawe makini.
***
Sebastian hakwenda tena chuoni mbali na hapo hakupata hata lepe la usingizi akawa anashinda tu hospitalini ili kujua maendeleo ya kipenzi chake.
Maendeleo ya Sonia yakazidi kuleta matumaini,akaanza kufumbua macho yake.Tayari alianza kupata fahamu,alivyopiga jicho pembeni yake alikumbana na sura ya Sebastian.
“Sonia,vipi hali?”
“Hapa wapii?”
Sonia akauliza swali kwa sauti ya chini huku akitizama huku na kule,haikumchukua hata dakika moja akajua ni sehemu gani alipo,picha iliyomjia harakaharaka ni ya Alhandro,akajikuta analia machozi yakambubujika na kulowanisha mashuka.
Alijisikia uchungu kupita kiasi,aliamini kwamba teyari keshabakwa lakini hakutaka kuyapa mawazo hayo kipaumbele.
“Sonia usilie nyamaza”
“Sebasti...ian,kwa...”
“Shss shsss..”
Hakuna kitu kilichoendelea hapo zaidi ya Sebastian kumtuliza,akapata kibarua cha kumbembeleza.
Daktari akafika akamchoma sindano nyingine ya dawa na kubadilishiwa bandeji kichwani,bado mdomoni alikuwa ana jeraha.

Lakini kadri siku zilivyozidi kupita ndivyo lilizidi kupona.Baada ya siku nne,akaruhusiwa kutoka hospitali.
Ulaya hakuwa na ndugu yoyote yule zaidi ya Sebastian ambaye ndiye alikuwa mtu wa karibu yake,kila sehemu waligandana.Ratiba ya Sonia ikajulikana kama sio Hostel basi yupo na Sebastian mjini tena kwenye migahawa tofauti tofauti.Bado alikuwa akimuimbia wimbo wake uleule wa kila siku NAKUPENDA, kama Sebastian angelikuwa mwanamuziki angeshalitoa 'album' hata nne.
“Sebastian wewe ni kama kaka yangu,siwezi naomba unielewe”
Hilo ndilo lilikuwa jibu la Sonia kila siku,aliogopa kujiingiza kwenye maswala ya mahusiano, tena ugenini mbali na hapo hakumjua vizuri Sebastian na ndiyo maana moyo wake ulikuwa unasita siku zote.
“Usiseme ivyo”
“Niseme nini sasa?”
“Toa hilo neno kaka,labda ndiyo utanielewa nina maana gani”
“Kuna course work sijamaliza kuifanya mwezi ujao tuna test,naomba tuongelee habari za masomo”
Msimamo wake ulikuwa huohuo kila kukicha,lakini pia ndani ya moyo wake alihisi kumpenda Sebastian alijaribu kuizua hali hiyo lakini alishindwa.
****
Wanaume wengi wa kizungu walikuwa wanamtupia macho kila kukicha,Mwalimu Emilia nayeye hakuacha kumuandama,alitaka wawe kama mume na mke japokuwa walikuwa wote ni jinsia moja,hilo ndilo swala lililomchefua kupita kiasi.
***
“Sebastian mfano siku nikikukubalia,utafanya kitu gani cha kwanza?”
“Yaani hata sijui kwa kweli,ila nitahakikisha kitu cha kwanza nyumbani wanakujua”
“sasa mbona swala hilo litakuwa mapema?”
“Mimi sitojali”
“Kwanini unanipenda sana?”
“Swali lako lina majibu milioni,lakini ni moyo Sonia”
“Ninakupenda Sebastian lakini moyo wangu unasita sana,bado sijakuamini”
Sebastian na Sonia walikuwa wakiongea siku hiyo jioni tulivu siku ya Jumamosi,hakukuwa na masomo kwao siku hiyo wakaamua kuitenga ili wazungumze kuhusu mambo yao mbalimbali huku wakitaniana,kila alichoongea Sebastian Sonia alikifurahia.
“Likizo hii utaenda nyumbani?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Sebastian.
“Ndio nitaenda”
“Naomba usiende”
“Mh.. kwanini sasa?”
“Nataka nikupeleke nyumbani kwetu Marekani wazazi wangu wakujue”
“Hapana bwana”
“Tafadhali nakuomba”
“Sasa nyumbani nitasema nini?”
“Waambie ukweli”
“Kwamba?”
“Upo namimi Sebastian”


*******
ENDELEA KUSOMA HADITHI NA SIMULIZI ZA MTUNZI….EMMANUEL F.KWAY(THE STORY MASTER)

0 comments:

Post a Comment

BLOG