Search This Blog

Sunday, May 31, 2020

MCHACHUKO SEHEMU YA 8/10



MCHACHUKO
MTUNZI….EMMANUEL F.KWAY(THE STORY MASTER)
AGE…(18+)
WatsApp…+255718 862176
SEHEMU YA 8 KATI YA 10
*******
 *******


Maisha yalianza kurudi tena kwenye mstari, kila siku Adrian hakuacha kumshukuru Jaqlin kwa kuyainua,

alijilaumu sana kipindi cha nyuma alivyokuwa anatumia pesa kwa fujo wenda angekuwa na Jaqlin kipindi cha Enzi zake basi angekuwa bilionea.
“Baby inabidi tununue kiwanja,tujenge hotel”
Jaqlin alikuwa ni mwanamke aliyewaza mbele, hakuridhika hata kidogo, usomi ndiyo uliomsaidia, kila hatua aliyofanya basi ilikuwa na malengo.
“Hizo pesa tutapata wapi?”
“Hii hiii gest yetu itazaa hotel,hata ikichukua miaka kumi lakini trust me,tutafungua tu, na ndiyo ndoto yangu ilikuwa tangu nasoma nije kumiliki hotel, naomba uniunge mkono”
“Unadhani mimi nitasema kitu jiniazi wangu”
“Nani jiniazi?”
“Wewe hapo”
“Sio kweli, bila support yako unadhani tungefika hapa?ni juhudi zetu wote Mpenzi wangu,na hotel ikiisha tu,naomba niwe mke wako rasmi”
“Baby una mikakati kuliko Bill gates, kuna ule msemo wa wazungu unasema every nini successful”
“Ha! Ha! Ha! Haaa! Every successful Man has strong woman behind”
“Ewaaa, mimi kipindi cha nyuma nilikuwa nawadharau sana wanawake niliwachukulia kama hawana lolote katika jamii”
“Sasa hiyo kauli itoe,usithubutu, wanawake tunaweza”
“Lakini mkiwezeshwa”
“Ha Ha Haaaaa”
Kwaa saa nzima waliongelea mambo yao mengi sana, hususani maswala ya kuongeza vitega uchumi,Jaqlin alikuwa ni mwenye akili ya kufikiria maisha hata siku moja hakupenda starehe japo mara kadhaa Adrian humuomba watoke.
“Leo twende club baby wangu”
“Umeanza Adrian, si unajua hizo sehemu mimi sipendi sana”
“Kwa leo tu jamani,nakuomba twende”
“Sawa,Mwanaume ushasema unadhani nitafanya nini,twende tukale tu bata”
“Ha ha ha ha”
Wote walifurahi.
Siku hiyo walinyuka pamba na kupendeza kisawasawa!
Walihakikisha Jovvana amelala kisha kuanza safari, Adrian mbele Jaqlin mpaka kwenye Starlet kisha
Kuingia ndani ya gari yao mpaka club.
Ulikuwa ni usiku wa saa tano ndipo walipoingia ndani ya lango la Club baada ya kulipa, walizama ndani na kupandisha ngazi, mziki ulikuwa mkubwa. Wazee kwa vijana walijichanganya katikati na kucheza mziki wa kizazi kipya,
wakiwa wameshikana viuno.Akili ya Adrian ilimrudisha katika maisha yake yaliyopita alivyokuwa akijirusha kipindi alivyokuwa anapenda vimwana!
“Baaaaby”
Jaqlin aliita kwa sauti kubwa kutokana na kelele za mziki kutokea kwenye spika.
Nyimbo iliyokuwa ikipigwa kwa wakati huo ilikuwa ya Oliva Ngoma.
Wanaume wengi walimtupia Jaqlin jicho wakimthaminisha, japokuwa alivaa kaptula ya jinsi iliyovuka magoti lakini alitingisha club nzima kwa uzuri wa kuvutia.
“BOSS I HAVE SEEN HER”(TAJIRI NIMEMUONA YULE MWANAMKE)
“ARE YOU SURE?”(UNA UHAKIKA)
“100%”
“I THINK YOU KNOW WHAT TO DO?”(NAFIKIRI UNAJUA CHA KUFANYA)
“YAH”
Ujumbe ulijibiwa kwenye simu kupitia barua pepe kisha mzungu huyo aliyekuwa kaunta kuanza kumuangalia Jaqlin,akitafuta njia ya kumpeleka chooni.
“I need shot”
Mzungu aliagiza na kupatiwa pombe kali kisha taratibu kupanda ngazi akimuendea Jaqlin,baada ya kumkaribia alijifanya amejikwaa na kummwagia pombe Jaqlin juu ya shati lake, lengo lake ni lilikuwa aende washing room huko ndipo angempata kisha kuikamilisha kazi ya Maxmilian aliyekuwa Uingereza akimsubiri Jaqlin kwa hamu sana.

“sorry Madam”
Alisema mzungu,Jaqlin alimtizama Adrian na kumuaga kuwa anaenda chooni kunawa, hakuelewa kuwa ameshaingia kwenye mtego.Mzungu aliyekuwa anamwangalia alipaka dawa kali za usingizi kwenye kitambaa chake na taratibu kuanza kumfuata Jaqlin kwa nyuma.

AGE….(18+)

****

Ilikuwa ni sherehe iliyohudhuriwa na watu wasiopungua elfu moja na mia mbili! na magari ya kifahari si chini ya mia tano katika jumba kubwa la Mzee Ahsan Abrahaman.
Ni kitendo cha mke wake kujifungua mtoto na kufikisha siku arobaini ndipo walipomtoa nje kumfanyia mahafali, ilikuwa ni furaha sana kwake, aliamua kufanya ivyo tu kwa sababu ya furaha aliyokuwa nayo, hakutaka kusherekea peke yake aliwaalika matajiri wenzake na lengo lake lilikuwa ni kuwaonesha kuwa Mungu anajibu maombi.
Mpaka siku arobaini zinafika mtoto alishapewa jina na kuitwa Raul, alikuwa mtoto mzuri mweupe na mwenye Afya njema, kila aliyemtizama alidhani wenda ni mtoto wa kike,lakini kilichomchanganya Mzee Ahsan ni rangi ya Raul, ngozi na nywele havikuendana kabisa na asili yao.Raul alikuwa ana ngozi ya kiafrika yenye kung’aa,Licha ya kuyaona hayo hakutaka hata siku moja kuufungua mdomo wake kumuhoji mkewe Hajrath kuhusu swala hilo,sababu alimuamini.

Kitendo cha kumuuliza swali hilo kingemaanisha kuwa alikuwa hana imani na mtoto na aliamini kingemkera mke wake.
Katikati ya jiji la New Delhi kulikuwa kuna heka heka tena nyumbani kwa Mzee Ahsan Abrahman,matajiri mbali mbali walizidi kufurika!Hajrath muda wote alikuwa akilia machozi hana raha jambo ambalo lilimshtua sana mumewe,alilia kwa kusema uwongo, moyoni alijiona mkosaji sana kwa kumdanganya mume wake,ki ukweli Raul hakuwa mtoto wa Mzee Ahsan wa damu, hakuelewa itakuaje kama mumewe atagundua siku moja.

Ilivyogota saa moja ya jioni Sherehe ilizidi kupamba moto.Mzee Ahsan alichukua kipaza sauti kwa Mc na kuonekana kuwa ana taka kuongea maneno machache ukumbi ulikaa kimnya.
“Kwanza namshukuru Allah kwa yote,namshukuru Pia Mke wangu Hajrath au Mama Raul,nampenda sana mke wangu,nimeamua kuwaita hapa nifurahi sana nanyi, kabla ya yote Mohamedi naomba ule mzigo”
MZEE Ahsan alikaa kimnya na kumgeukia kijana mmoja wa kihindi mwenye ndevu kiasi aliyevalia kanzu nyeusi, kisha kusogea mbele na kiboxi kidogo, kisha kumkabidhi Mzee Ahsan,kilivyofunguliwa kila mtu alitoa macho yake, zilikua ni funguo ndogo zenye rimoti,Mzee Ahsan alirudi nyuma kidogo na kufungua pazia jekundu.
Kila mtu alikodoa macho yake, lilikua ni gari la garama ambalo hata India halikufika,Mzee Ahsan aliamua kumnunulia mke wake HAMMER III ORIGINAL kama zawadi ya kumpatia mtoto ambaye atakuja kurithi mali zake,Lilikua ni gari la kisasa pana lililokaa kama boxi.Watu walizidi kupiga makofi na yowe.
Hajrath alizidi kulia machozi, alimsikitikia sana Mume wake kwa kufanya jambo hilo,Lakini hakuwa na jinsi alisogea na kumkumbatia huku akizidi kulia kwa uchungu.
“Usilie Mke wangu,Hiyo ndiyo zawadi yako,nitakutafutia na dereva awe anakupeleka popote unapotaka kwenda,nataka kesho jioni twende tukapumzike uingereza kuna rafiki yangu amenialika kule”
“Na…kupen..da sana Baba Raul”
Hajrath alijikaza na kumwambia mume wake.Watu walikunywa na kusaza siku hiyo, ilipofika mishale ya saa saba kila mtu alitawanyika makwao na wengine kudiriki kusema kuwa Mzee Ahsan alifanya kufuru ya mwaka.

Mzee Ahsan hakuwa mtu wa longolongo kesho yake asubuhi Benz tatu zilifika katika jumba lake kwa safari ya kuelekea uwanja wa ndege kwa ajili ya safari ya uingereza kisha wakitoka hapo waende Los Angeles Marekani.
Alikuwa ni mwenye furaha iliyozidi kifani moyoni.Hajrath alipanga mizigo yake haraka haraka na wafanya kazi kufika na kuichukua na kuiweka ndani ya gari,kila kitu kilivyokuwa sawa walifunguliwa milango huku wakiwa na Raul mkononi kisha Mabenzi kuondoka mpaka uwanja wa ndege Mumbai,
hapo walifunguliwa milango na kuelekea kwenye Ndege kubwa na kusubiri safari ianze baada ya dakika thelathini.
“Are you okay Darling?”
Mzee Ahsan alimuhoji mke wake baada ya kumuona ni mwenye wasiwasi sana.
“Yes am fine Sweetheart”
“I love you”
“I love you more”
Hajrath alimjibu Mume wake lakini moyoni alikuwa ni mwenye wasiwasi mwingi,alishindwa kuelewa itakuwaje endapo Raul akianza kulia na angetakiwa kumnyonyesha.
siku zote humnyonyesha na kikopo chenye maziwa maalumu ya watoto bila mume wake kujua.Vitu vingi vilitiririka ndani ya akili yake na kumkosesha raha ya safari.Hajrath alikuwa ni kama amejichawia mwenyewe kwa kuwaza habari hizo, sababu Raul alianza kulia kwa sauti kubwa ndani ya ndege na kumfanya azidi kuingiwa na wasiwasi mwingi.
“Raul anataka kunyonya,tafadhali mnyonyeshe”Mzee Ahsan alisema.
Hajrath alikuwa ni bado mwenye wasiwasi na kuelewa kuwa muda mfupi ataenda kugundulika,alizidi kujawa na Mashaka, majasho mengi yalimtoka. Raul alizidi kulia kwa sauti kubwa mpaka muhudumu wa ndege kusogea kwenye viti vyao.

***
MAXIMILIAN hakuweza kumsahau Jaqlin hata kidogo, sura ya mwanamke huyo mwenye ngozi ya kiafrika ilimpagawisha vibaya mno.Alivyotua Uingereza tu alianza kufanya mikakati ya kumtafuta Binti huyo na kumuita mlinzi wake ofisini kwake.
“I want to send you somewhere Carlos”(nataka kukuagiza mahali Carlos)
“ where My boss?”(wapi tajiri yangu)
Maximilian alimuelekeza Carlos na kumkabidhi tiketi ya ndege la shirika la Air India akamuulizie Jaqlin ni wapi aliposhukia na kumtafuta.
Baada ya siku mbili Carlos alianza safari na kufika mpaka Mumbai, hapo alikaa takribani wiki nzima kwa ajili ya upelelezi, alishapewa picha ya Jaqlin kupitia Camera za CCTV zilizokuwa uwanjani hapo,na kuambiwa kuwa yupo Hospitali ya Appolo na waudumu wa ndege.
Taarifa za kuonekana kwa Jaqlin zilitumwa mpaka Uingereza kwa Maximilian na kuonekana kufurahishwa na habari hizo.
“Sasa tunafanye bosi?”
“Kuwa mpole kwanza,fanya mambo taratibu usikurupuke hata kidogo!fanya fanya kwanza uchunguzi wa kina ili tujue itakuaje,huku mimi nitaanda ndege ndogo ikiwa tayari nitakutaarifu,ukiishiwa pesa niambie”
“Sawa mimi nakusikiliza wewe hapo,mimi sina neno lolote la kuongeza juu yake,hii kazi ni ndogo kwangu”
“Unijulishe kila hatua utakayo piga”
Mazungumzo yao yaliishia hapo yakimuacha Carlos akiwa nje ya hospitali akimtizama Jaqlin akitembea huku na kule,
hata yeye alikiri kuwa mwanamke huyo ni mzuri sana, japokua alikuwa ana mimba kubwa teyari!
Carlos alizidi kufanya uchunguzi wake, kila asubuhi alifka hospitali ya Apolo, nia yake ilikua ni kumuweka Jaqlin karibu na aweze kumfuatilia kila sehemu aendayo.

Mpaka siku Jaqlin anarudi Tanzania Carlos alikuwepo ndani ya ndege wanasafiri pamoja bila Jaqlin kujua.Alivyofika Mbeya Mwakaleli pia walishuka wote.Jaqlin hakuelewa lolote!
Siku zilizidi kuyoyoma bado Carlos alikuwa akimfuatilia Jaqlin.
Siku hiyo Carlos aliamua kwenda Club ili kuosha macho na kuwaangalia warembo wa Tanzania,alivutiwa na Wanawake wa kitanzania kwa uzuri,na kudiriki kusema kuwa “Tanzania ina vimwana”.
“Heii Muzuuuunguuu”
Mwanamke mmoja aliyevalia kimini kifupi na kuyapandisha maziwa yake alijigonga baada ya kumuona Mzungu ameketi mwenyewe.
“Hello Pricess”
“Hiii,yes I am fine,I just me want you to buy me to buy a beer then you is take me Marekani”
Mwanamke alizidi kujigonga akitaka ofa ya bia kutoka kwa mzungu akiongea kiingereza kibovu lakini Carlos alimuelewa na kumnunulia Bia.
“What is your name?”
“Magreth,Naitwa aah am Magreth”
“My name is Carlos”
Macho ya Carlos yalitua kifuani mwa Magreth na macho yake kuonekana kumtamani kimapenzi, ni kweli suruali yake ilituna kwa Mbele, Magreth aliliona hilo na kumsogelea kisha kuanza kumpapasa.
“Huyu lazima nimpe mambo anipeleke ulaya”
Magreth aliwaza hayo na kuendelea kukishika kifua cha Carlos mpaka mwenyewe alipotaka watoke nje kwenye giza wakamalizane kikubwa!

Walipofika nje nyuma kwenye Giza Magreth alitoa ndizi ya mzungu na kupiga magoti kisha kuanza kuinyonya, Carlos alidata. Alihema juu juu huku akihisi raha za ajabu.
Mpaka ataoa oil chafu alikua haamini, Alimvuta Magreth na kuanza kumnyonya mdomo wake wakibadilishana mate kwa njia ya Ulimi.
Walihaidiana kuwa kesho yake wakutane club usiku tena muda huo huo.
Carlos akawa amenogewa na hako kamchezo, na kusahau kilichompeleka.

**
“Boni”
“Sema?”
“unapigiwa mwanangu?”
“Kivipi?”
“Mkeo anagongwa na mzungu Fulani hivi”
“Nani Magreth?”
“Sasa una wake wangapi? fala nini!kuna mzungu kila siku anapiga”
“Muongo Jona,unanitania”
“ sasa si unabisha,leo usiende shifti usiku ukajionee. Mwenyewe club”
“Club gani?”
“pale Tripple D”
Boni alijisikia uchungu ajabu, habari hizo zilimpandisha Mori! alimpenda sana Magreth, moyo wake ulijawa hasira,na misuli yake kukakamaa.
Alikuwa ni mwenye mwili mkubwa na misuli yake kujigawa kama mcheza filamu wa marekani RAMBO, alikuwa ni mwanaume wa shoka aliyepanda hewani futi nyingi, kifua chake kilijigawa na kufanya kiwe kama makalio ya mtoto wa miaka kama mitatu hivi,ndani ya akili yake aliwaza kuuwa alimpenda sana Magreth,siku hiyo alivyorudi nyumbani kwake asubuhi alilala na kuamka jioni akimuaga mke wake anaenda kazini huko kiwandani.

Magreth ndoto yake alitaka itimie, alishaelewa nini maana ya Marekani ilikuwa ni lazima ampagawishe Carlos na apelekwe nchini Marekani, hakuelewa kuwa mume wake yupo ndani ya club hiyo na anamuona kila anachokifanya.

Walipigana madenda kwa fujo na kurudi ndani ya club wakiwa wameshikana viuno kimahaba.
“Wait baby” (Nisubiri Mpenzi)
Carlos alisema.
“okay”
Carlos alisimama baada ya kuiona Sura ya Jaqlin na kuhama siti, aliwatizama na kuanza kufanya mazungumzo na Maximilian aliyekuwa uingereza.
Alipaka dawa zake na kumuendea Jaqlin kisha kummwagia pombe.
Kila hatua aliyopiga, Boni alimtizama na kumshuhudia anaingia katika vyoo vya wanawake.
“Ina maana huyu kamfata Mke wangu chooni, nauwa wallahi”
Aliwaza Boni akiwa ameshika chupa kubwa mkononi ya wisky na yeye kuingia choo cha wanawake.
Carlos alipotaka kumziba Jaqlin na kitambaa puani kilichokuwa na madawa alihisi maumivu mengi kichwani, hakukaa sawa alibebwa na kutupwa chini puu na Boni.
Mzungu alikaa sawa, alirusha ngumi lakini ilidunda kifuani mwa Boni,Jaqlin alivyoona hali hiyo alitoka mbio, na ndiyo ilikuwa ponea yake hakuelewa kuwa muda mfupi angekuwa mateka,alitoka nje na kwenda kumuita Adrian.
***
Carlos alikuwa katikati ya kundi la watu wamemzunguka huku akiwa ameshikwa na Boni kohoni anavuja damu puani na meno yake matatu yapo chini sakafuni, alilia kwa uchungu kwa sababu ya kipigo alichopokea kutoka kwa Boni aliyekuwa mwenye uchungu wa mke!
“Nini ongea Kiswahili leo mpaka utaongea Kiswahili ku** la Mama yako, sorry nini”
“Noo just a…m sorry,wh..at have I done?I haven’t done anything wrong(Hapana.Nisamehe,nimefanya nini?sijafanya kitu chochote kibaya)
Wengi wao walimuonea huruma Mzungu aliyekuwa akipigwa chooni,lakini Adrian ndiye aliyeoneshwa kuguswa zaidi, aliingilia kati kwa lengo la kumsaidia.
“Kaka yaishe ndugu yangu,msamehee utatafuta kesi bure, usikute shushushu huyo”
“Hapana ndugu,huyu muda mrefu nilikuwa namlia timing,blaza inauma sana,huyu ni mwizi wa mke wangu,lazima nimfunze adabu huyu mzungu, akaadithie Marekani,”
“Punguza jazba hasira hasara,Embu njoo tuongee”
Jaqlin nayeye alikuwa nyuma nyuma, aliingiwa na huruma kiasi cha kutamani kulia na alitamani ampe msaada Carlos lakini hakuwa na sauti.Jaqlin na Adrian walimuombea msamaha Carlos na kutaka wamchukue ili wampeleke hospitali.
Mpaka wakati huo Carlos hakuwa ana uwezo wa kusimama mwenyewe, ndipo Jaqlin alipomfuata na kumuinua kwa safari moja tu kumpeleka Hospitali, hakuelewa kuwa anamshika mtu aliyetumwa amteke.


***

“OndoKa nimekwambia”
“Naomba unisamehe Mume wangu,nipo chini ya miguu yako”
“Nitakuuwa ujue humu ndani unipe kesi,toka Mage usinitie kichefuchefu”
“Boni tafadhali niurumie,nitaenda wapi usiku wote huu?”
“Nenda kwa mzungu wako,naingia chumbani nikitoka nisikukute. Nadhani unanielewa vizuri huwa sirudii mara mbili nikishaongea kitu,sitaki kukuona tena ndani ya hii nyumba”
Boni alijawa na hasira kama Chui aliyejeruhiwa na Mkuki mbavuni,moyo wake uliumia kupindukia kwa kitendo cha kumfumania Mke wake na Mzungu club. Kitendo hiko kiliufanya moyo wake usitake kumuona tena Magreth mbele yake,Baada ya kutoka kumpiga mzungu sasa hasira zake zilihamia kwa mkewe.Aliingia chumbani huku nyuma akiacha ujumbe kuwa asimkute Magreth seblen awe ameshaondoka.
“Bado upo?”
Aliuliza Boni baada ya kutoka chumbani.
“Mu..me wa..ngu”
Boni alikuwa ni mwanaume mwenye msimamo kimaisha, akishaamua kitu basi ni vigumu kumbadilisha mawazo,hakujali kuwa ni usiku mnene kiasi gani, alimtoa Magreth nje na kumtupia mabegi yake kisha kufunga mlango.
Magerth alilia machozi ya uchungu, hakuelewa maisha yake ataishi vipi, hakuwa na ndugu wala wazazi. Alikuwa ni mtoto yatima,Boni ndiye alikuwa kila kitu kwake, alitamani mambo yabadilike lakini haikuwa ivyo.Alijilaumu kwa kutokuwa muaminifu kwenye ndoa.
***
Carlos aliendelea kupata matibabu na garama zote zilikuwa chini ya Jaqlin na Adrian. walimuonea huruma mzungu huyu aliyedai alikuja bongo kufanya utalii kisha baadaye kupigwa vibaya mno.
Hakuna hata mmoja aliyeelewa kilichomfanya Carlos awepo Mbeya Mwakaleli, hata siku moja.
Usoni muda wote alikuwa akitabasamu lakini adhma yake ilikuwa ni kumteka Jaqlin na kumpeleka uingereza kwa Maxmilian.
“How do you feel now?”(hali yako vipi sasa)
Jaqlin alimuuliza Carlos asubuhi baada ya kufika hopitalini.
“Atleast am okay”(nina afadhali)
Matibabu yaliendelea mpaka ilivyofika wiki moja Carlos aliruhusiwa kutoka hospitalini.
Adrian na Jaqlin walimuomba sana waishi naye lakini Carlos hakutaka kuwa mrahisi kwa mara ya kwanza ili asigundulike, lakini mwishowe alikubali.
Hatimaye akawa anaishi na Adrian pamoja na Jaqlin nyumba moja.

Ujenzi wa Hotel ulizidi kuendelea, Adrian akawa ana jukumu la kusimamia kila ujenzi unavyoendelea,baada ya mwezi mmoja gorofa tatu kwenda juu zilikuwa zimekamilika, lengo lilikuwa gorofa nne.Carlos mara kadhaa alikuwa akishirikishwa kwa kila hatua.
Hawakuelewa ni kitu gani anakiwaza, lakini kila akikumbuka wema wanaomfanyia rohoni ilimuuma sana, alijua Jaqlin hakustaili kutekwa. Licha ya yote hakuwa na jinsi ilikuwa ni lazima afanikishe dhamira iliyomtoa Uingereza.Mawasiliano baina yake na Maximilian yalizidi kufanyika chini kwa chini akimpa kila utaratibu unaoendelea.

****
Gari nyingine ilinunuliwa hili lilikuwa la Jaqlin,tayari walikuwa wana magari mawili ya kutembelea, pesa zilianza kumiminika kwa kasi,Wateja walikuwa hawakauki baa ,kwenye gest mpaka katika migahawa yao.
Adrian na Jaqlin walifurahia sana, maisha yalianza kurudi kwenye mstari taratibu.Walimpenda sana Jovvana kuliko kitu chochote kile na tayari walianza kumtafutia mwalimu awe anamfundisha taratibu sana.
Kwa makadirio ya hapo Mwakaleli A & J Lodge ndiyo iliyoongoza kujaza wageni kuliko nyumba ya wageni yoyote ile.
Walidiriki kusema kuwa Mungu yupo pamoja nao,na mtafutaye hachoki, juhudi za Jaqlin zikawa zimemuinua tena Adrian kiuchumi.
Shirika Tanrod liliitwa kutengeneza barabara na madaraja. Wazungu takribani Hamsini waliingia Mkoani Mbeya Mwakaleli na kuomba kuonana na mmiliki wa A & J Lodge,walitaka kuikodi kwa miezi kumi na mbili mpaka kazi yao ya ujenzi itakapo kamilika. Adrian na Jaqlin waliitwa na kuongea na mkandarasi Mkuu wa kichina Chung Wii ili wakamilishe mkatabata wao.
Chung Wii alihitaji nyumba nzima kwa miezi kumi na miwili kwa shilingi dolla laki tano za kimarekani. Adrian na Jaqlin hawakutaka kuyaamini masikio yao hata kidogo mpaka pale makaratasi yalipoletwa na kusaini mkataba wa pesa hizo.
Hakukuwa na utani, pesa ziliingizwa kwenye akaunti zao, zilikuwa ni pesa nyingi mno kwa kipindi watakachokaa wajenzi wa kampuni ya Tanrod.
“Thank you Mr.Chung Wii”(Shukrani Mr.Chung Wii)
“It is okoi it okoi”
Mchina alijibu kwa Kiswahili kibovu akijaribu kuwajibu.
Pesa hizo hawa kutaka zikae kwenye akaunti, haraka haraka walipandisha Hotel yao. kwa pesa walizokuwa nazo ujenzi ulikamilika kwa kipindi kifupi sana na pesa iliyobaki wakanunua Canter ya mizigo,kila kitu walikipanga kwa akili sana, ujio wa Chung Wii ukawa umefanya ukombozi wa maisha yao kiuchumi.
Hazikupita hata wiki walitafuta gari kubwa aina ya Canter ya kufanyia biashara,mambo kwao yalienda haraka haraka.
“Ulikumbuka tuliongea nini Darling?”
“Mambo mengi tuliongea Jaqlin”
“Kuhusu hotel kuisha”
“Ndoa?”
“Sasa kumbe nini, Hotel yetu ikiisha nataka unioe Adrian, sitaki kuishi kihuni sawa?”
“Hilo sio la kuuliza Mama watoto”
Waliongea wakiwa ndani ya Canter. Adrian akiwa analiendesha kulipeleka Mjini Mwakaleli ili wamkabidhi kijana aanze kazi.Siku zote hawakuwahi kumsahau Mzee Mwangenya hata siku moja. walikuwa wakimtumia pesa kila mwisho wa Mwezi nayeye aliwapa Baraka zote alifurahi sana.
Baada ya kufika Mwakaleli Mjini walionana na Paul mtoto wa baba yake mdogo na Adrian.
“Sasa Paul”
“Naam Anco”
“Hili canter utakuwa unapiga ruti hapa Dar es saalam na Morogoro,naomba uwe mwaminifu maana sitoshindwa kukunyang’anya, nimekupa hili gari kwa makusudi, sitaki uwe mtoto wa kijiweni wewe ni ndugu yangu, utakuwa unajipatia riziki.sawa?”
“Sawa Anco,nitafanya ivyo”
“kila ruti utakayopiga utaniambia mimi au Mama Jovana”
Paul akawa amekabidhiwa gari kubwa la mizigo aina ya Canter.
****
Carlos siku zote aliwaza kuteka tu, lakini moyo wake ulisita kufanya zoezi hilo, kutokana na kuoneshwa mapendo yote na Adrian pamoja na Jaqlin.
Moyo wake ulimsuta na ndiyo maana zoezi hilo lilikuwa gumu kwake siku zote.Kila alipoulizwa na Maxmilin kuhusu ni wapi alipofikia hakuwa na jibu lililojitosheleza!
“You son of a bitch. what is wrong with you? why are you taking so long?”(Wewe mtoto wa Malaya tatizo lako nini,mbona inakuchukua muda mrefu)
“I was sick sir, that is why I couldn’t make it”(Nilikuwa naumwa Mkuu,ndiyo maana nikashindwa kufanikisha)
“Stupid! don’t you ever tell me again your non sense,have you heard?”(Mjinga,kamwe usinieleze upuuzi,umenisikia)
“Yes boss”
“I need her within a Month,Understood?”(Namuhitaji ndani ya Huu mwezi.Umeelewa)
“Yes sir”
“Good”
Mambo yalianza.
Baada ya kukata simu na kufokewa na bosi wake akawa hana jinsi zaidi ya kwenda duka la madawa na kutafuta vidonge vya valium vingi sana ili aweze kumnywesha Jaqlin kwa njia yoyote ile.
Asubuhi ya siku iliyofuata alifika anapoishi Jaqlin na Adrian kisha kugonga.
“Oooh Mr. Carlos get in”
Jaqlin alimkaribisha kwa Furaha Carlos huku mkononi akiwa ana viatu vya Jovana, ilionekana alikuwa katika heka heka za kutoka.
“Jovvana msalimie Anco”
“Chikamooo”
“Sema GoodMorning”
“GuchMorning”
Jaqlin alionesha uchangamfu sana kupita kiasi.Carlos alimuonea sana huruma sababu alishaelewa ni kitu gani anaenda kukitenda muda mfupi ujao, ni siku hiyo hiyo ilibidi awe ameshamteka na kumpa taarifa Maxmilian aliyekuwa uingereza.
Jaqlin alitembea mpaka jikoni na kutengeneza chai ya mgeni na kumkabidhi Carlos.
“I have problem Jaqlin”(nina tatizo)
“Tell Me my friend”(Niambie rafiki yangu)
“Am leaving today,can you take me to Songwe airport please,I have an Emergence"(Ninaondoka leo,unaweza kunifikisha uwanja wa ndege wa Songwe tafadhali,nina dharura)
Carlos alidanganya na alishajua kazi anayotakiwa kuifanya mbele yake,Kwa kuwa alizoeleka Jaqlin hakuwa na kipingamizi chochote kile.
“First wait,let me talk to my husband"(Kwanza subiri niongee na mume wangu)
Jaqlin alitoa simu na kumtafuta Adrian hewani sababu hakuwepo asubuhi hiyo,alishaondoka kwenda kusimamia ujenzi wa hotel.
“Ndio ni Carlos..Nitamuacha Jovana kwa babu yake si ndiyo leo nilikuwa nampeleka…ndio mpenzi wangu..ha ha ha acha wivu wako basi.. ndiyo nitakuwa makini Lov, nakupenda Mume wangu mtarajiwa Mwaa mwaa mwaa mara elfu nane Haha ha ha ha ha sawa,nikimpeleka tu nitarudi.Nitakupikia ndio.sawa baadaye nitakupigia”
Adrian akawa ametoa ruksa. Huruma yake ikawa imemponza, hata siku moja hakuwahi kumuwazia Carlos mabaya katika maisha yao tangu aanze kumjua, alikuwa mzungu mpole na mwenye kuongea na kila mtu.

Jaqlin alivaa haraka haraka na kumvalisha Jovvana na wote kunyoosha mpaka kwenye gari ndogo iliyokuwa nje.Carlos muda wote alimtizama Jaqlin na kumuonea huruma sababu hakujua nini kitakacho mtokea masaa machache yajayo.
Walifunga mikanda na safari ya kwenda kwa Mzee Mwangenya kuanza na baadaye waende Songwe kama Carlos alivyotaka iwe.
**
“Oyaa changamka,pandisha hizo ngazi Mudi,vipi hujala?”
“Nimekula Bosi”
“Mbona unakuwa kama goigoi,changanya zege hilo”
Adrian alikuwa saiti akisimamia ujenzi wa hotel akijaribu kuwaelekeza wafanyakazi.
Wote walimfurahia hakuwa bosi mkali, alikuwa ana urafiki na kila mtu.
Jioni ilipofika kazi iliisha na kuwasha gari mpaka nyumbani kwake ili akapumzike.Lakini alipofika nyumbani ukimnya ulimshangaza sana, hakusikia sauti ya Jaqlin wala Jovvana Mpaka jioni hiyo,hakutaka kuwa na wasiwasi, alipitiliza mpaka chumbani na kuoga kisha kuanza kula huku akitoa simu yake na kumtafuta Jaqlin hewani,simu iliita lakini haikupokelewa.
“Mhhhh..labda atakuwa njiani,yaani huyu mwanamke akiwa anaendesha gari tatizo lake ndiyo hilo hapokei simu”
Hayo yalipita kichwani mwa Adrian.
Mpaka inafika saa sita ya usiku Jaqlin hakutuma meseji wala kupiga simu, akawa amesimama nje kuliangalia kila gari, alipiga tena simu ya Jaqlin bila kupokelewa.
“Au kapata ajali?,ngoja nimpigie Mzee”
Alivyopiga Simu ya Baba yake Mzazi hapo hapo ilipokelewa, tena akiwa katika hali ya uchovu uliochanganyika na hasira.
“Nini usiku usiku?”
“Mzee samahani kwa usumbufu”
“Una tatizo gani kuna msiba?”
“Hapana Mzee wangu, Jovvana yupo kwako?”
“Ndiyo yupo,kuna shida gani?”
“Mama yake ndiyo alimleta?”
“Ndiyo,vipi kwani?”
“Mama yake hayupo kwako Mzee?”
“Maswali gani unaniuliza hayo?Kaja hapa kasema anaenda Songwe na Yule rafiki yako Mzungu”
“Sawa Mzee Usiku mwema”
Adrian hakutaka kujifikiria tena.Hisia za Jaqlin kupata ajali ndizo zilianza kuzunguka ndani ya kompyuta ya ubongo wake.
Aliwasha gari kwa safari ya kwenda Songwe ili aangalie njiani kama kuna gari lililopata ajali.
Umbali kama wa kilomita Thelathini aliona gari lipo kando ya barabara,moyo ulimwenda kasi, lilikuwa ni gari ndogo aina ya Vitz nyeusi, aliitambua ilikuwa ni gari la mpenzi wake Jaqlin.
Taratibu nayeye aliegesha gari lake nyuma yake kisha kushuka.
Moyo ulizidi kumuenda kwa kasi hasa alivyoona hakuna watu ndani ya gari na Simu ya Jaqlin ipo juu ya kiti cha mbele.
Alielewa wazi kuna kitu kimetokea na tena kibaya sana.

 ******

“Maziwa yamekauka Mume wangu sijui nitafanya nini?”
“Sasa kwanini hukuniambia Mama Raul mpaka tunaingia ndani ya ndege?”
“Hata mimi sikuelewa na sikujua kama hili swala lingetokea, hapa nilipo nimechanganyikiwa nashindwa cha kufanya huwezi ukaongea na wahudumu wa humu nipate maziwa ya mtoto hata ya makopo?”
“Hapo itakuwa vigumu ndege ishaanza kutembea,labda sijui. lakini inabidi niongee na wahudumu wa ndege tuone itakuwaje?”
“Sawa wanaweza kutatua hili tatizo”
Mzee Ahsan hakuwa na la kufanya zaidi ya kusubiri ndege ikae sawa angani kisha kufungua mkanda wa siti na kumuendea muhudumu wa ndege,Raul alizidi kupiga kelele akilia sana, dalili zilionesha kuwa alikuwa ana njaa na anahitaji maziwa.
“Mke wangu amekaukiwa maziwa ya kumnyonyesha mtoto unaweza kunipa msaada?”
“Mmmh.hapa itakuwa vigumu labda tuombe abiria mwenye maziwa ya akiba akitokea mwenye uungwana basi atakuwa amewasaidia,nenda kakae ili nitoe hilo tangazo”
“Sawa nitashukuru”
Mzee Ahsan alirudi kitini huku akiomba dua awepo abiria mwenye maziwa ya kopo.
Wote wawili walikuwa wakimuonea huruma Raul aliyekuwa akilia kwa sauti sana huku majasho yakimtoka.
Sauti ya kipaza sauti ilisikika kutoka kwa Muhudumu wa ndege akiomba msaada wa maziwa ya kopo.
Mwanamke mmoja wa kizungu aliyekuwa na mtoto mchanga aliingiwa na huruma na kuguswa na mtoto aliyekuwa akilia,alifungua begi lake kisha kutoa kikopo kilichojaa maziwa kisha kumkabidhi muhudumu wa ndege.
Mzee Ahsan hakuamini alimshukuru sana.

Raul alinyamaza kimnya baada ya kupewa maziwa ya kopo, mpaka wanatua uwanja wa ndege wa Otawwa Canada Raul alikuwa amelala fofofo.Ilikuwa imegonga majira ya saa kumi na moja alfajiri hapo waliingia kwenye ndege nyingine ya shirika la uingereza na safari nyingine kuanza.
Mzee Ahsan akawa amejawa na furaha sana baada ya kuhitimisha safari yao, alionekana kuchoka, yeye na mkewe hawakuwahi, Kusafiri kwa umbali mrefu kiasi hicho.Walianza kutoa mabegi yao mpaka nje ya uwanja wa ndege huku akitizama huku na kule,akiwaangalia wageni waliokuja kumpokea.
“Mr and Mrs Ahsan welcome to UK”
Maneno hayo aliyasoma juu ya kibao kilichoshikwa na kijana mrefu kiasi,alimuendea na kumshika begani.
“Am MR.Ahsan”
“Ohh your Welcome,this way sir”
“Thank you”
Wote waliongozana na kijana huyo aliyeonekana kutumwa na Mwenyeji wa Mzee Ahsan,waliweka mizigo yao ndani ya Taxi kisha kuanza safari ya kuelekea mji wa Cassini kilomita kama thelathini kutokea uwanjani hapo.
“How is india?”
Alivunja ukimnya dereva taxi.
“How do you know we are Indians?”
“My boss told me”
“Okay,India is good,India is very good country”
“But here!no peace,this country is very dangerous”(Lakini hapa,hakuna amani,hii nchi ni hatari)
Gari lilizidi kusonga mbele huku Dereva akizidi kuwazoea wageni aliowachukua kutokea uwanjani, alionekana ni dereva mchangamfu sana.
Hatimaye Wakawa wamekata kilomita ishirini.Walikunja kushoto na kunyoosha moja kwa moja.Mzee Ahsan alishangazwa na utulivu wa nchi hiyo, japokuwa alikuwa tajiri kupindukia lakini hiyo ndiyo ilikuwa siku yake ya kwanza kufika katika nchi hiyo.
Ubaridi wa wastani ndiyo uliyomvutia zaidi.Taxi ilisimama nje ya geti kubwa na refu kwenda juu na dereva kufungua kioo cha gari kisha kutoa kichwa chake nje,Camera na vipasa sauti ndiyo vilikuwa vinaongea, nyumba hiyo ililindwa na technolojia ya hali ya juu sana.

Baada ya kuonesha sura mlango ulijifungua na uwazi kuonekana,Uwanja mkubwa sana ulionekana ukiwa umepambwa na bustani ya maua yaliyokatwa vizuri,Walizidi kusonga mbele kama mita mia hivi ndipo walipoona jumba kubwa linalo fanana na ngome ya Mfalme, ilikuwa nyumba kubwa ajabu yenye eneo la hekari mia moja na kuzidi.
Walinzi maalumu walikuja na kuwafungulia milango.
Nje ya Mlango alisimama mwanaume mrefu wa kibritish akiwa anatabasamu.
“Ahsan Abrahaman my friend”
“Alexander”
Wote walishikana mikono na kukumbatiana kwa furaha kisha baadaye kusalimiana na Hajrath.Wote walifurahia.

Taarifa za kuwepo kwa tajiri Ahsan Abrahaman katika nchi hiyo zilisikika na walitaka kumfanyia unyama ili wamtoe pesa, kikundi kilichoitwa Black kidnappers kilichojishughulisha na utekaji wa watoto matajiri kiliingia kazini.Ni dereva taxi ndiye aliyetoboa siri kuwa Mzee Ahsan na mke wake walikuwa na mtoto mdogo ivyo walianza kufanya mikakatati yao.
Kilikuwa ni kikundi kilichomilikiwa na tajiri mfanyabiashara aliyeishi Uingereza lakini makazi yake yalikuwa London.
Vijana walitumwa waanze kazi mara moja tena bila kupoteza muda.
Wanawake watatu warembo wakavalishwa ushungi ili waingie ndani ya jumba kubwa la Alexander.
Kutokana na kuwepo kwa ulinzi wa uhakika hawakufanikiwa, ilibidi wasubiri siku nyingine.
***
“Itabidi kesho nikawatembeze baharini huko,mkatembee tembee na Raul”
Alisema Alexander usiku wa siku hiyo.Ngozi ya Raul ya kiafrika ilimshtua Alexander, mara nyingi alitamani kuhoji lakini hakudiriki kufanya ivyo mpaka aliposubiri Hajrath aondoke ndipo alipomuuliza Mzee Ahsan.
“Huyu mtoto ni wako?”
“Ndiyo Alexander”
“Mbona hana asili ya kwenu?”
“Mke wangu ana ndugu zake, babu wa babu yake alikuwa muafrika ndiyo maana ikawa ivyo”
“Nimeuliza tu usinifikirie vibaya,sasa mimi naenda kupumzika kesho asubuhi kama nilivyowaambia”
“Sawa usiku mwema”
Wote waliagana na Ahsan kwenda kupumzika na mke wake Ili kusubiri kesho kukuche!

Kulivyokucha Alexander alimuamuru dereva wake waanze safari ya kuelekea kwenye fukwe za bahari.Hajrath alifurahishwa na safari hiyo na muda wote akawa katikati ya mikono ya mumewe na pembeni akiwepo Raul,kabla ya hapo walipitia kwenye maduka makubwa ya matajiri wakiwa wanaosha macho,jioni ya saa kumi walianza safari ya kwenda katika fukwe za bahari.Hawakuelewa kuwa nyuma wanafuatiliwa na watekaji wa kundi la Black kidnapers na lengo lao lilikuwa ni kumchukuwa Raul wakiamini kuwa wakimteka mtoto huyo watakuwa wamevuna pesa.
Lilikuwa ni kosa la jinai kwa Mzee Ahsan,Dereva pamoja na Alexander kushuka ndani ya gari na kumuacha Hajrath akimbadili nguo Raul.Hapo ndipo wanawake wawili walipotokea upande wa pili na mwanaume mmoja.
Walimpulizia dawa Hajrath puani na kumfanya apoteze fahamu zake, hapo hapo walimchukua Raul na kutokomea naye.

***
Adrian alizidi kuchanganyikiwa sio masihala,Kitendo cha kuliona Gari la mpenzi wake limetelekezwa kando ya barabara kilimfanya azidi kuingiwa na hofu nyingi! Akili yake iliganda na kushindwa kuelewa ni kitu gani kimetokea.
Alijuwa wenda Jaqlin atakuwa yupo mahali Fulani jirani lakini hakujua ni wapi,aliingia ndani ya gari na kuanza kuliondosha taratibu sana huku akitupa macho yake huku na kule bila ya mafanikio ya kumuona Jaqlin,alifika Mpaka Uwanja wa Ndege wa Songwe na kushuka akitizama huku na kule.Alijaribu kuipiga Simu ya Carlos pia ilikuwa ivyo ivyo.Wazo lililomjia tena ni kurudi alipolikuta gari la Jaqlin.Baada ya kutembea kwa gari mita mia tatu themanini simu yake ya mkononi iliita alivyoingalia alikutana na namba ngeni.Aliitizama kwa muda na kuipokea.
“Adrian mpenzi wangu”
Sauti ya Jaqlin ikawa imemshtua sana upande wa pili wa simu,alikuwa ni kama mtu anayehema.
“Uko wapi Jaqlin?”
“Nipo Hospitali”
“Hospitali?Kwanini?umeumia?una tatizo gani na upo hospitali gani?”
“Hospitali ya Songwe naomba uje tafadhali”
Adrian aliuzungusha usukani na kurudi Kaskazini alipotokea.Baada ya nusu saa aliweka gari kando nje ya hospitali ya Songwe na kushuka,Alitembea kwa haraka sana.
Jaqlin alivyomuona tu alimrukia na kuanza kulia.
“Vipi mbona upo hapa?”
“Carlos”
“Yuko wapi?”
“Carlos alitaka kunifanyia kitu kibaya sana”
“Kwanini na yuko wapi?na ilikuwaje?”
Sekunde chache Jaqlin alifuta machozi yake kisha kumtizama Adrian.
“Tulivyotoka Kwa Baba tukawa tunakuja Songwe uwanja wa ndege alipotaka nimsindikize,baadaye tukasimama sehemu ili tule,baada ya hapo akatoka kwenda kuninunulia soda,akanipa,kwanza sikunywa.Alinisisitiza sana niinywe,
“Tukaanza safari ya kuondoka baadaye kufika katikati ya safari gari ikazima,kuna kijana akaja kutusaidia na kwa kuwa nilikuwa sijabeba pesa nikampa ile soda anywe,haikupita hata dakika mbili Yule kijana akadondoka nikashtuka sana,nikashindwa kupata jibu la haraka”
“Yaani huyo kijana akadondoka?”
“Subiri Baby,alivyodondoka, kumuamsha hakuamka,ilibidi tutafute gari ingine kwa msaada,tulivyomfikisha hapa ikadaiwa kwamba alikunywa kinywaji chenye dawa,nilivyomtafuta Carlos sikumuona tena,mimi nina mashaka naye,alitaka kunifanyia kitu kibaya”
Katika maelezo aliyotoa Jaqlin moja kwa moja Carlos alichukuliwa ndiye muhusika namba moja, kutowepo kwake ndiyo ukawa mwanzo wa kumuhisi.
“Darling inabidi tuwe makini sana”
Masaa matano baadaye kijana aliyekunywa dawa iliyochanganywa na vidonge vya valium alishtuka akiwa amechoka mno.Hapo Jaqlin akawa amepona tena kwa mara ya pili.
****
Kadri siku zilivyozidi kwenda ndipo walizidi kusahau. Jaqlin na Adrian walizidi kuendelea kufanya ujenzi wa hotel yao,Adrian hakutaka kumuacha Jaqlin nyuma, kila wakati alikuwa naye.Baada ya miaka miwili kufika Hotel ikawa tayari imekamilika na kusubiri siku ya uzinduzi rasmi na hapo walitafuta nyumba jijini Dar es saalam ili wakaanze maisha yao huko.
Walikuwa tayari matajiri waliomiliki Canter tano,Canter moja ikawa imeleta nyingine! Kilichokuwa kinasubiriwa hapo ni ndoa peke yake.Bahati nzuri walisikia nyumba inauzwa na Mzee wa Kiswizi aliyekuwa Dar es salaam kwa kazi ya mkataba, ilikuwa ni nyumba kubwa mno yenye kila kitu ndani maeneo ya Oysterbay.Mzee huyo wa kiswizi aliwakabidhi jumba hilo kwa bei rahisi, taratibu za kukabidhiana nyumba zilikamilika na kilichokuwa kinasubiriwa hapo sio kitu kingine ni harusi kubwa.

Jovvana alishakuwa teyari na aliweza kuongea na muda wote alikuwa ni mwenye furaha pengine kuliko mtoto yoyote Yule duniani, alijiona ni mwenye bahati kuzaliwa na wazazi waliompenda na kumjali muda wote.
Jumba lilikuwa kubwa tena ya gorofa tatu kwenda juu,ilikuwa na uwanja mkubwa wenye kuingiza magari hata thelathini, uwani kulikuwa kuna uwazi mkubwa na nje kulikuwa kuna bwawa la kuogelea.
“Baby hii nyumba bab kubwa”
Jaqlin alivunja ukimnya wakizidi kuzunguka na Adrian, alishangazwa sana,mpaka inafika jioni hawakumaliza kuzunguka kila sehemu.
“Hii nyumba sio mchezo,sijapata kuona Jaqlin,lakini hii rangi sijaipenda”
“MIMI nimeipenda iache ivyo ivyo usitake kuharibu vitu”
“Aya mama”
Wote walirudi ndani.Baadaye walitoka kwenda kutafuta vitu vya kula usiku kisha kurudi.
Jaqlin aliiingia jikoni na kupika kisha wote kuanza kula.

Usiku ulipoingia walimlaza Jovvana chumbani kwake na wao kuingia ndani. Kitendo cha kuingia chumbani kwao walianza kupigana madenda kwa fujo huku wakivuana nguo zao kwa haraka,kila mtu alikuwa ana mori iliyochanganyika na furaha.Jaqlin udhaifu wake ulikuwa kwenye maziwa Adrian alilitambua hilo, alimtoa nguo yake ya juu ya kuanza kumnyonya maziwa yote mawili kwa zamu,likitoka la kushoto basi linafuata la kulia.
Mihemo ilizidi kutoka katika pua za Jaqlin huku akizidi kujinyonga.Mambo yalikuwa mwake Adrian alimbeba Jaqlin na kumbwaga kitandanni kisha kupanda juu yake akiendelea na zoezi lake la kumnyonya maziwa huku mkono wake mwingine ukiwa unacheza na ikulu,jaqlin alikunja kunja mashuka huku akiwa ameyafumba macho yake, alihisi raha za ajabu mno.
Alikuwa katika Sayari nyingine ya huba, hakika Adrian alimuweza.
“Assshss B……abyyyyyyyy Assssh na…kupenda”

 Mambo yalikuwa mukide mukide kwa wote wawili kifupi walikuwa katika sayari nyingine ya huba,waliridhishana kisawasawa na mara kadhaa katikati ya mchezo Jaqlin hutaja swala la ndoa.Baada ya masaa matatu wote wawili walijifunika shuka moja, Jaqlin akiwa ameweka kichwa chake kifuani mwa Adrian na kudiriki kukiita ni kitanda chake.
***
Asubuhi kulivyokucha Adrian akawa ana kazi ya kupiga simu juu ya magari ya mizigo ni wapi yalipofikia, kwa kipindi hiko alikuwa akitaka idadi kamili ni kiasi gani yanaingiza,lengo lilikuwa ni kuanza kupiga hesabu za harusi yao,alitaka kufanya harusi kubwa itakayotishia jiji.
Adrian ni mwanaume wa Kinyakyusa aliyependa sifa kama muhaya na alitaka kuwafunga midomo waliosema kuwa alifulia,alivyowakumbuka marafiki zake waliomtosa kipindi ana dhiki alitabasamu mwenyewe.
“Sasa mbona unacheka mwenyewe Mpenzi wangu,utakuwa chizi ujue”
Jaqlin alitokea kwenye ngazi na kumkalia Adrian katikati ya miguu yake huku akimbusu midomoni.
“Kuna kitu nimekumbuka ujue,ndiyo maana ukanikuta nafurahi,kipindi nilivyofulia kuna washkaji zangu nilikuwa nikila nao starehe huwezi amini walinikana,sasa hivi navyokwambia nafikiria harusi tutakayofunga nataka itingishe Dar es salaam nzima”
“Mume wangu una sifaaaaa”
“Nataka niwaoneshe kuwa bado jina Chif lipo palepale,nataka nikufanyie harusi kubwa ushangae”
“Mhh yangu macho”
Siku mbili nzima walikuwa wakizungumzia juu ya namna watakavyo fanya harusi yao,lakini kabla ya yote ilibidi kwanza wazindue Hotel yao iliyokuwa Mbeya Mwakaleli, waliyoipa jina la JJ HOTEL ilikuwa ni hotel kubwa yenye kila mahitaji ndani yake,ilijengwa kisasa na vifaa vya ndani viliagizwa kutokea china kuanzia scrin mpaka vyoo na makabati.

Kabla ya kupanda ngazi chini kulikuwa kuna kaunta ya pombe kali na pembeni kulizibwa na vioo vyeusi huko walipaita Club ndogo waliyoingia V.I.P ambapo mziki laini ndiyo ulitumbuizwa.
Ilikuwa Hotel yenye ubora na sio ya kitoto.Ndani ya wiki tu jina lilianza kuvuma kila kona,kila mtalii akifika ni lazima afikie JJ HOTEL walidiriki kuiita ni hotel ya nyota tano Mkoani hapo Mbeya.
kila mtu aliizungumzia,Mapaparazi walishaanza kumsaka mmiliki wa hotel hiyo na kuanza kumfatilia na kugundua kuwa ni kijana anayemiliki vitega uchumi vingine,walivyompigia hesabu ikagundulika kuwa ndiye tajiri wa tatu kijana nchini Tanzania wakiongozwa na Joackim akifuatiwa na Abdallah Aziz.
Kila mtu alitaka kumjua kijana huyu Adrian anafanana vipi.Adrian alikuwa tishio jingine la jiji hasa baada ya kununua BMW X6 na Jaqlin akitembelea RANGE ROVER sport magari hayo yaliagizwa ndani ya siku moja! Maisha yalizidi kuwanyookea, walizidi kuwekeza pesa kwenye magari makubwa, hatimaye wakanunua magari ya makontena mawili yaani semitera.Hiyo ilizidi kuwapandisha chati, Adrian alipanda na kuwa tajiri namba mbili.
Mpaka mwaka mmoja unapita utajiri wao uliongezeka mara tatu zaidi, hii ni kutokana na juhudi zao hawakuchoka kutafuta na siku zote alimshukuru Jaqlin sababu ndiye alikuwa nyuma yake akimshauri.

Mpaka mwaka unaisha Adrian alikuwa ni miongoni mwa vijana matajiri nchini Tanzania alikuwa tajiri sio masihara.
Jaqlin alikuwa kama malkia kila sehemu aliyopita aliheshimika, alikuwa ni miongoni mwa wanawake wenye bahati mno.
Na kupewa jina Mke wa tajiri, Range rover sport aliyotembelea ilikuwa ya kisasa na kipindi hiko ilikuwa moja tu Dar es salaam nzima.
Adrian alizidi kupeta na waliomcheka walitamani ardhi ipasuke ili wakimbie aibu.
“Aaaah chif,vipi ndugu yangu?”
Mwanaume mmoja mrefu alitoa salamu hiyo, alimtizama na akili yake kumrudisha siku aliyokuwa hana pesa na mwanaume huyo jinsi alivyomkana, leo hii ana muita huku akimkenulia meno.
“Safi tu vipi?”
“Ndugu ulikuwa wapi siku nyingi sana sijakuona”
“Maisha tu,ubize bize sana”
“Basi naomba tutafutane Chif”
“Sawa nitakutafuta”
Wakati anaongeleshwa akili yake haikuwa hapo hata kidogo, maneno aliyoongeleshwa yalipita sikio ya kulia na kutokea kushoto.
Alikuwa akimsubiri Jaqlin atoke kubadili nguo ndani ya duka kubwa la nguo la My fair, walikuwa katika harakati za shoping kisha kesho yake wasafiri kwenda Arusha,nia ya safari yao ilikuwa ni kwenda kwa wazazi wake na Jaqlin.
“Baby hapo vipi?”
“Hapo bomba ila hilo gauni si ungetafuta ndefu kidogo livuke magoti si unajua tunaenda kwa wazazi alafu uliwatibua”
“Eti eeeh!”
“Ndiyo maana yake”
Siku zote Jaqlin alikuwa ni mwanamke mwenye furaha, alijivunia sana kuwa na Adrian licha ya kuwa matajiri lakini alikuwa ana amani sana na siku zote alijihisi mwenye furaha mno kuliko mwanamke yoyote Yule duniani.
Taratibu walishikana mikono huku Adrian akiwa mkononi amebeba furushi la mfuko mpaka ndani ya Bmw x6 na kuingia kisha kuanza safari ya kurudi kwao Oysterbay.
“Baby”
Jaqlin alimuita Adrian gari lilivyoanza kuondoka.
“Niambie Malkia”
“Sasa mbona harusi unaisogeza mbele kila siku?”
“Nina maana yangu,utaelewa mke wangu”
Nia ya kusogezwa harusi mbele ilikua ni kwasababu ya maandalizi.Adrian alikuwa akifanya mawasiliano na watu mbalimbali ndani na nje ya nchi, lengo lake lilikuwa ni harusi yao itingishe jiji zima la Dar es salaam,Adrian hakutaka kumwambia Jaqlin lolote.
kwa ujanja aliokuwa nao aliweza kuwasiliana na muandalizi wa harusi maarufu aliyekuwa Afrika Kusini jijini capetown, Msafiri Dome! bila kumwambia Jaqlin lolote!
“Harusi ni mwishoni mwa Mwaka huu mwezi wa kumi na mbili,twende kwanza tukasafishe nyota yetu kwa wazazi wako”
“Sawa baby, lakini inabidi twende na Jovvana unajua siwezi kumuacha nyuma”
“Inabidi tumuombee Ruksa,sasa leo jioni nitafanya utaratibu wa tiketi ya ndege kesho tuanze safari”
Moyo wa Jaqlin ukawa umetulia alivyosikia habari za ndoa yake,walifika kwenye jumba lao saa kumi ya jioni na hapo ndipo walianza kufanya mawasiliano na mwalimu wa shule ya East Africa International School Madam Angelina Massawe!
“Sawa Mama Jovvana hakuna neno, lakini tu awahi kurudi shule ili aendelee na masomo yake”
“Hilo ondoa shaka Madam Angelina hata wiki hatutofikisha”
“Hakuna shida”
Mwalimu akawa amekubali na kilichosubiriwa ni Adrian jioni hiyo arudi na Tiketi tatu za ndege kwa ajili ya safari.

Jaqlin na Jovvana walikimbia getini na wote kufungua geti baada ya kusikia honi za gari walikuwa ni wenye furaha ya safari.waliona masaa hayaendi.
“Pole Baba Jovvana,tiketi ulipata?”
“Tiketi ninazo,zipo ndani ya begi saa tatu kesho,msichelewe”
Adrian alishuka na kupokelewa begi, Jovvana alimrukia baba yake na kubembea kwenye mikono yake huku akichekelea,siku zote alimpenda sana Baba yake!
“Nimekuletea chocolate”
“Kweli Dad?”
“Ndio”
Jovvana alifurahi.Walivyoingia ndani alijitupa juu ya sofa kubwa huku akitupia macho runinga.
“Alafu ulisoma magazeti ya leo?”
Adrian alimuuliza Jaqlin.
“Hapana,vipi kwani?”
“Leo tumetolewa,ile jana kumbe tulipigwa picha na mapaparazi,pale nilivyokuwa nakufungulia mlango wa gari”
“waliandikaje?”
“Utawaweza. basi tu ili wauze”
Jioni ya siku hiyo Jaqlin alikuwa ana kazi ya kupanga nguo zake na Adrian pamoja na Jovvana, aliwaza sana, alikumbuka pesa alizomuibia Baba yake kipindi yupo Arusha na sasa alitaka kuzirudisha na aombe msamaha kisha waanze vikao vya ndoa mara moja,ni miaka mingi sana ilipita bila ya kuonana na wazazi wake na aliamini kuwa walimtafuta vibaya mno.
*****
Saa moja kamili Jaqlin alikuwa macho akipiga pasi nguo za Adrian kisha baadaye kuandaa chai,kila kitu kilivyokamilika waliingia kuoga na kumuamsha Jovvana kisha wote kujumuika Mezani kunywa chai.
Nusu saa ilivyokatika taxi iliyotoka mwalimu Nyerere uwanja wa ndege ilifika nje ya geti na kupiga honi.
“Jamani jamani twendeni,jamaa kafika tayari,Jovvana tangulia mbele,usisahau kufunga mlango Mpenzi wangu”
“Baby nimesahau kitu”
“Umeanza sasa”
“Hapana ngoja kidogo fasta fasta”
Jaqlin alivyotoka,wote waliingia ndani ya Taxi iliyokuwa tayari nje inawasubiri.Safari ilianza mara moja ya uwanja wa ndege.
Kitendo cha kufika tu ndiyo zilibakia dakika kumi peke yake ilikuwa kidogo wachelewe lakini waliwahi.
Dakika ishirini baadaye walikuwa juu angani wanaangalia dunia kwa chini, Ndege ilikuwa teyari inapasua mawingu.Badaa ya dakika hamsini walitua uwanja wa KIA Arusha na ndiyo hapo safari yao ilikomea.
Hakukua na haja ya kusubiri zaidi ya kuchukua usafiri mpaka Kwa Wazazi wa Jaqlin.Nyumba ilikuwa imejawa ukimnya wa hali ya juu, ilionekana hakuna watu lakini Jaqlin alizunguka Nyuma na kumuona Mama yake anamwagilia bustani ya maua.
“Jaqlin”
“Maamaaa”
Badala ya Mama kukasirishwa alimrukia binti yake na wote kudondoshana chini kwa furaha,alikuwa ni kama mwanampotevu.
Baba mzazi aliyekuwa ndani amepumzika kelele zilimshtua hata yeye alipomuona binti yake alitabasamu na kukumbatiana.
“Ulikuwa wapi mwanangu?”
Baba aliuliza.
“Wazazi wangu naomba mnisamehe na..”
Jaqlin alivyotaka kupiga magoti Mzee alimzuia na kumuinua juu.
“Hauna haja ya kuomba msamaha mimi na Mama yako tulikutafuta sana.Tunashukuru tumekuona na una afya nzuri,tulihangaika sana,sahau yaliyopita na sahau yote tumekusamehe”
Adrian alikuwa hajasema lolote na aliwatizama huku akiwa na Jovvana Mikononi.
Wazazi walimfuata na kumlaki kwa furaha,hakuna kilichofuata hapo zaidi ya Mbuzi kudondoshwa na kuliwa siku hiyo hiyo.
Usiku wa siku hiyo ili bidi waeleze kilichowafungisha safari.Wazazi hawakuwa na kipingamizi walifurahi hasa baada ya kumuona Mjukuu wao Jovvana alikuwa mtoto mzuri na mnene kiasi,hii ilitokana na matunzo ya kizungu aliyolelewa na wazazi wake,Jovana hakuwahi kusikia harufu ya mihogo wala viazi tangu afike Dar es salaam alikuwa akila soseji,baga pamoja na Hotdog!
“Babu nataka Hotdog”
“Hoto dogoo ndiyo kitu gani tena mjukuu wangu?huku hakuna hoto dogo”
Adrian na Jaqlin waliangua vicheko mpaka wakadondoka chini, mzee hakuweza kusema Hotdog neno lilikuwa ngeni kwake.Waliendelea kula nyama choma baada ya hapo walienda kulala usiku ulipoingia,kilichokuwa kina subiriwa hapo ni harusi peke yake Jaqlin aliona siku hazisogei kuanzia siku hiyo.


 ******

Alikuwa ni mwanamke mrembo sio utani,macho yake makubwa yaliwapagawisha matajiri mbalimbali,shepu ndiyo usiseme,ngozi ndiyo kabisa!wanaume walishindwa kutegua kitendawili cha asili ya mwanamke huyo,sababu alikuwa akiruka nchi mbali mbali za kitajiri, makazi yake yalikuwa ni Saudi Arabia,lakini mara nyingi huonekana nchi kama ufaransa na Marekani jijini Miami.Alikuwa mrefu wa wastani na mwenye ngozi nyeupe ya kung’aa, sura yake ilikuwa ya duara na akicheka basi dimpoz huonekana,Mwendo wake alijua kuutumia kisawasawa na nyuma alikuwa ndiyo gumzo,kalio lake lilibinuka na kutengeneza kimlima fulani,vimini alivyokuwa anavaa vilizidi kuwa kivutio kikubwa sana kutokana na mvuto wa ajabu aliokuwa nao kwenye mapaja na mguu wake kupewa supu.

Lakini uzuri wake ndiyo alitumia kama mtaji katika maisha yake, mpaka kulala naye ni lazima uache sio chini ya dolla laki moja tena hiyo ni kwa siku moja.Alikuwa ni Mwanamke tajiri mno,ukimwangalia usingethubutu kusema kuwa ni changudoa mwenye kuuza mwili wake,ungemuona ungesema kuwa ‘mwanamke ndiye huyu’ kumbe yupo kimaslai zaidi.
“I think you know why you’re here Babra?”(Nafikiri unajua kwanini upo hapa Babra)
“Yeah I have been told Mr.Maxmilian”(Ndiyo niliambiwa Mr.Maximilian)
Babra alijibu kwa mapozi na kuyazungusha macho yake na kumfanya azidi kuwa mzuri,lengo la kutua Nchini South Afrika lilikuwa ni kumsikiliza Tajiri Maxmilian na inavyosemekana alitakiwa kesho yake apae mpaka Tanzania Mkoani Mbeya Mwakaleli,lakini hakujua anaenda kufanya nini na ndiyo maana alitokea Saudi Arabia mpaka Afrika Kusini ili kusikiliza wito.
Habari za Babra zilimvutia sana Maxmilian na alichukizwa sana na utendaji kazi wa Carlos baada ya kurudi na kumwambia kuwa alishindwa kufanya kazi.
“Nataka kukutuma huko Tanzania,mimi sijawahi kufika, kuna kijana nilimtuma akashindwa kufanya kazi,kuna mwanamke nina muhitaji anaitwa Jaqlin ana mchumba wake,fanya juu chini uharibu kila kitu na hiyo ndiyo itakuwa njia rahisi”
“Hiyo ni kazi ndogo tambua unaongea na mwanamke gani?tambua unaongea na mrembo wa dunia,huyo mwanaume wa aina gani ambaye atatoka kwenye mtego wangu? labda awe hanisi,lakini kama ni lijali,nitafanya achukiwe na mchumba wake na ikishindikana nitatumia vijana wangu ili kazi iwe rahisi”
“Ha ha ha ha ha ha ha ha ha,kwanza kabla ya kuondoka nahitaji nionje penzi lako”
“Dolla laki tatu mpaka kesho asubuhi,utaniingizia kwenye akaunti”
“Hizo siyo pesa kwangu,nitakuongeza,nataka unipe vitu motomoto”
“pigia mstari”
Wakati mazungumzo hayo yanaendelea macho ya Maxmilian yaligota juu ya maziwa ya Babra, yaliyokuwa yapo nusu nje, yaani Boomz na kufanya ndizi yake ianze kufurukuta.
Waliongea mengi na kupanga mikakati itakavyokwenda na jioni kuelekea Capetown kwenye hotel kubwa ya nyota tano gorofa namba tisini na saba.
Babra hakuwa mzuri wa nje peke yake hata kitandani alikuwa hodari sio masihara,alimkatikia Maxmilian vibaya mno kama aliyeambiwa anaenda kufa kesho,aliweza kumiliki mchezo kwa nusu saa nzima bila kuchoka kifupi Maximilian alipelekwa puta kitandani.
“Kumbe hauna afya?”
Aliuliza Babra akiwa juu ya kifua cha Maxmilian.
“Nipo kwenye dozi ndiyo maana, ila nina kasheshe mimi”
Maxmilian alijitetea ili kuondoa aibu.
“Mhh mhhh.. ah wapi,hakuna mwanaume atakayeweza kunimiliki nikafurahi bado sijaona tangu nianze hii kazi,na akitokea basi na kazi nina acha anioe siku hiyohiyo”
“Acha utani”
“Ndio nakwambia tena”
“Unatakiwa kuondoka kesho mchana kwenda Tanzania nitakuingizia pesa kwenye akaunti yako,nampenda sana huyo binti sio utani,hata ikiwezekana nikakae naye mbali kabisa yaani nipotee naye nimfungie sehemu”
“Sawa usijali,sasa huyo binti nimfikishe wapi?”
“Tutawasiliana kama sio hapa Afrika kusini basi England”
“Ondoa shaka”
Wote walikubaliana na asubuhi iliyofuata pesa nyingi ziliingizwa ndani ya akaunti ya Babra kwa ajili ya kazi itakayo mkabili mbeleni,alikuwa ana usongo wa kufika Tanzania sababu ni nchi aliyohadithiwa kuwa ni ya amani na upendo.

Jinsi alivyovaa na kupendeza ilifanya Maxmilian amtamani tena kingono.Kweli mwanamke huyo alikuwa mzuri kupindukia,ungebahatika kumuona usingeamini kama kuna warembo kiasi hiko duniani.
Saa saba ya Mchana alikuwa teyari amewasili Capetown uwanja wa ndege kisha kupungiana mikono na Maxmilian.
Ndege iliacha ardhi na kuinua matairi yake angani, Babra akawa yupo safarini kuelekea Tanzania na ramani iliyomuelekeza mpaka hotel atakayo fikia JJ HOTEL ,iliyomilikiwa na Adrian pamoja na Jaqlin na ndiyo dhumuni lake lilikuwa kukutana na watu hao wawili kwa njia yoyote ile.
Saa mbili ya usiku alikuwa ametuwa uwanja wa Songwe Mkoani Mbeya baada ya kubadili ndege kutokea uwanja wa Mwalimu Nyerere Dar es saalam.
Alivyokuwa akitembea alifanikiwa kugeuza macho ya wanaume hata baadhi ya wanawake wenzake walimshangaa kwa jinsi alivyokuwa mrembo na mwenye mvuto.
“Excuse me,do you know this hotel?”(samahani,unahifahamu hii hotel)
Babra alimuuliza dereva Taxi aliyekuwa uwanjani hapo huku akitoa karatasi na kumkabidhi.
“JJ HOTEL? yes,lets go”
“How much will it cost to take me there?”(Ni kiasi gani cha pesa kunifikisha hapo)
“Fifty thousand Tanzanian shillings”(Elfu hamsini za kitanzania)
Dereva Taxi alimbangua Mgeni sababu ya lugha,Kwa kuwa Babra alikuwa ameshachenji pesa zake ilibidi akubali tu,Safari ilianza mara moja,walitumia masaa mawili na nusu kufika na Babra akashuka kisha kumlipa Dereva Taxi.
Hapo hapo alipokelewa na wahudumu mpaka ndani ya Hotel ya JJ na kupewa chumba, hata yeye alivutiwa na huduma za hapo,kila alichotaka alipewa dakika hiyo hiyo.
Baada ya kukaa siku mbili na kuzoeana na baadhi ya wahudumu ilimbidi amuulizie mkurugenzi wa hotel hiyo.
“Adrian na Jaqlin ni mtu na mchumba wake”
“Ndiyo wamiliki wa hii hotel?”
“Ndio”
“Wao wapo wapi kwa sasa?”
“Wapo Dar es salaam ndiyo wanaishi huko”
“Huku huwa hawaji?”
“Huwa wanakuja kupumzika kila mwisho wa mwezi lakini sidhani kama mwisho wa mwezi huu watakuja”
“Kwanini?”
“Wanafunga ndoa,mwishoni mwa Mwezi huu”
“Mhh hilo ni jambo zuri sana”
“Ndiyo ivyo,mimi nimepewa kadi ya watu wawili lakini rafiki yangu amesafiri”
“Kwaio tunaweza tukaenda wote?”
“Poa itakuwa vizuri pia”
Linda alishajenga urafiki na Babra kutokana na kiingereza chake kilivyooka,kila baada ya kazi huenda chumbani kwa Babra ili kujua habari za nje ya nchi sababu alitamani siku moja nayeye atoke nje ya Afrika,huo ndiyo ukawa mwanya wa Babra kujua kila kitu juu ya Jaqlin.

****
Maandalizi yalikuwa makubwa mno, bajeti iligharimu pesa isiyokuwa chini ya milioni mia tano za kitanzania na bado watu walizidi kuchanga, Mkurugenzi wa Kiwanda cha bia TBL alitoa kreti mia moja na hamsini za bia na katoni mia moja za pombe kali,akawa amebaki Mbunge wa Afrika Mashariki Mh.Abasi Kibasile yeye alitoa shilingi milioni tano na makosta hamsini na mbili kwa ajili ya wageni na gharama za chakula alisimamia yeye.
Harusi hiyo ilikadiriwa kuwa na watu wasiopungua elfu moja na mia mbili hamsini,wageni kutoka nje ya nchi ndiyo kabisa.

Adrian muda wote alikuwa ni mwenye heka heka,akishika hiki ana acha kile ilikuwa mbili wala tatu hazikai,kifupi harusi ilimtia kiwewe sababu alionesha kuipania na kuwa mwenye usongo.
“Baby utachanganyikiwa hata kabla ya harusi”
“Kwa kweli! maana nashindwa kuelewa,nguo za harusi nimeagiza Dubai mpaka leo hazijafika lazima nichangayikiwe,mtafute Linnah Mfugale muulize vipi Magari yale ya harusi itawezekana?”
“Niliongea naye jana usiku kasema poa”
“Afadhali baby,tiketi ishirini za ndege zile ushazituma Mwakaleli kwa Mzee?”
“Ndiyo nafanya utaratibu”
“Jaqueeee! tangu jana mpenzi?,wale wazee wanatakiwa wawahi kufika kwa ajili ya kufanya mila zao”
“Baby naenda kutuma sasa hivi”
“HAKUNA kutoka nje mtume kijana aende”
“Mhhh kazi ipo”
Kuanzia siku hiyo Adrian hakumruhusu Jaqlin wake atoke nje ya geti alikuwa kama Mwali,vikao vya harusi vilikamilika teyari, Kitchen part kilipita na sendoff kufanyika,kilichokuwa kinasubiriwa ni ndoa ya Adrian na Jaqlin.
Magazeti mbalimbali yaliandika habari za harusi,kila mtu alitaka kushuhudia ni wapi harusi hiyo ya tajiri kijana nambari moja Tanzania ingefanyika kwa namna gani?.Mzee Mwanganya alikuwa akicheka na mapengo kuonekana nje kila wakati akiwa amevimba na wazee wenzake na kujivunia kuwa na mtoto tajiri kama Adrian, kila mzee alimuheshimu,sababu ndiyo Mzee aliyekuwa na nyumba kubwa hapo Mwakaleli ya matofali na Ng’ombe wengi, yote hayo Adrian ndiye aliyefanya.

Babra na Linda walikuwa teyari wapo jijini Dar es salaam na kufikia Rombo Hotel shekilango wakisubiri harusi kesho yake saa tisa alasiri.
Minong’ono ya chinichini ilisikika kuwa harusi hiyo haitakuwa na mfano wake na ingekuwa funga mwaka.
Hatimaye yalibaki masaa machache harusi ifungwe, Adrian alikuwa na mpambe wake ndani ya jumba lake usiku, Jaqlin akiwa yupo kwa ndugu zake ili kesho wakutane kanisani.
“Mr.Ndama mbona nahisi tumbo linaniuma?”
“Hizo ni presha za ndoa, najua una hofu kidogo. kusimama pale mbele sio mchezo,inakubidi kidogo uzimue konyagi ndiyo upate confidence lakini kama sio mzoefu itakula kwako”
“kwani wewe kwenye ndoa yako ndivyo ulivyofanya?”
“Sasa kumbe nini,niligonga Konyagi kama glass tatu nikawa fiti,kila mchungaji atakalo sema mimi naenda naye sawa,hata hiyo kesho lazima nile mvinyo”
“Itabidi namimi nipige mtungi kwanza”
Peter Ndama ndiyo alikuwa mshenga wake,kuanzia kupeleka posa kwa Mzee Mshana mpaka barua, kila kitu alisimamia yeye.Urefu wao uliendana na ndiyo maana akamchagua yeye pamoja na mke wake ili waweze kufanikisha zoezi la ndoa kutimia.
****

Limo nyeusi za milango sita tatu, ziliongozana huku pembeni kukiwa kuna mapikipiki meupe makubwa,msafara huo haukuwa tofauti na wa malkia Elizabeth wa Uingereza.Limo ya pili ndiyo alikuwepo Adrian Mwangenya na Mpambe wake huku ya mbele ikiwa imebeba Wazee na nyuma wakwe zake ilikuwa ni heshima kubwa.
Muda wote Adrian alikuwa amechangamka kutokana na Konyagi glass nne alizokunywa asubuhi hiyo.
Ulikuwa ni msafara uliyonyamazisha kelele za boda boda na daladala,kifupi barabara zilikuwa kimnya zikitizama msafara huo,wengi walihisi ni ugeni kutokea nje ya nchi,
Costa Tisini na mbili zilikuwa nyuma zinapiga kelele zimebeba watu,msululu ulikuwa ni mrefu vibaya mno,magari yalikuwa ya kifahari.
Safari yao ilikomea nje ya kanisa kubwa la St.Joseph lililokuwa posta kisha mlango wa Limo wa nyuma kabisa kufunguliwa.
Adrian alikuwa katika muonekano tofauti,suti nyeupe aliyovaa ilimkaa sawasawia,muda wote alitabasamu na kuwa kivutio kwa watu,taratibu alitembea na mpambe wake mpaka mbele,kanisa liligubikwa na kelele,waliomfahamu hawakutegemea kuwa leo hii anaoa.wengi walijua ni maigizo kumbe ndiyo ukweli wa mambo kicheche anaoa.Walivyofika mbele walisimama na kilichokuwa kinasubiriwa ni magari ya bibi harusi kutokeza ili ndoa ifungwe,lakini mambo yalikuwa kinyume mpaka nusu saa inakatika bibi harusi hakuonekana.
Adrian alianza kuingiwa na wasiwasi na kuendelea kusubiri, zilipita tena dakika tano nyingine bila dalili yoyote ile.
“Adrian vipi tena?”
Peter Ndama Mpambe alimuuliza Adrian kwa sauti ya chini baada ya kuona dalili hiyo.
Kanisa lilikuwa kimnya, Adrian alishaanza kuingiwa na wasiwasi sana.Mmoja mmoja alianza kuinuka kanisani na kutoka nje,dalili zilionesha kuwa hakuna ndoa tena.Ghafla walisikia kelele za matarumbeta nje ya kanisa.
“Haooo”
Adrian alipiga kelele kwa furaha na kukimbia nje huku Mshenga wake akiwa nyuma yake,hakuamini alipomuona Jaqlin yupo ndani ya shela tena juu ya farasi mweupe na mpambe wake nyuma alikuwa ni kama malkia siku hiyo.


*****

Mzee Ahsan Abrahaman alikuwa amechoka na hana furaha, mkononi alishika kiasi cha dolla laki tisa na hamsini kwa ajili ya ukombozi wa mwanaye wa kiume Raul,hata siku moja hakuwahi kujua kuwa sio mwanaye wa kumzaa hakuelewa kuwa mtoto huyo aliibiwa kutoka Hospitali ya Appolo na aliitwa Jovan, uaminifu aliouweka kwa Mke wake Hajrath ndiyo uliofanya asiwe hata na mawazo hayo.

Leo hii anatoa kiasi cha shilingi dola laki tisa, pesa hizo hazikuwa kitu ukilinganisha na thamani ya Raul kwake.
Hakuwa peke yake aliwashikirisha wapelelezi kutoka FBI na ndiyo ushauri aliopewa na Alexander.Askari walikuwa wamevalia nguo za kiraia na walikuwa mita mia moja kutoka aliposimama Mzee Ahsan aliyekuwa chini ya gorofa kubwa anasubiri maelekezo ya kukabidhiana pesa na kupewa Raul.
Jambo hilo lilikuwa likiangaliwa kwa umakini na askari kutoka FBI.
“Grii griiii”
Simu ya Mzee Ahsan iliita na kuiweka sikioni.
“Umefika?”
“Ndio”
“Una mzigio wetu?”
“Niko nao”
“unaliona hilo basi hapo?”
“Ndio”
“Ingia ndani”
Kila aliloambiwa Mzee Ahsan alitii na hapo aliingia ndani ya basi kubwa.
Majambazi wa Black kidnappers hawakuwa wajinga walielewa kuwa ni aina gani ya mchezo hatari wanafanya, nia yao ilikuwa ni kujua kama mzee huyo alikuwa amefika na askari,ni kweli waliona gari nyeusi inaondoka kwa kasi ikifuata basi aliloingia Mzee Ahsan.
Hilo ndilo kosa walilofanya askari wa FBI.Mzee Ahsan alizungushwa nusu saa nzima mpaka basi lilipofika mwisho na kumwagiza kuwa atafute Taxi,yote aliyokuwa anafanya walimuona.
Black Kidnappers walikuwa wamejikamilisha na kulikuwa kuna watu maalumu wa kucheza na Camera za CCTV, kamera zote za mjini walizihack na kuweza kuzitumia katika mitambo yao.
“Unaona hiyo chemba iliyokuwa wazi?”
“Ndio nimeiona”
“unatakiwa utumbukize fasta pesa na uondoke”
“Sasa na mwanangu?”
“Tumbukiza Mzee”
MZEE Ahsan alitembea na kutumbukiza briefcase ndani ya chemba,askari wa FBI walivyofika baada ya dakika moja hawakuweza kuambulia kitu chochote, pesa zilikuwa teyari zimeshaondoka na Mmoja wa kundi hilo aliyekuwa chini na kuzichukua akiwa na pikipiki.
Baada ya masaa mawili walisikia kuna mtoto aliyekuwa juu ya gorofa la Mai Plazza ametelekezwa,walivyoenda kumuangalia waligundua kuwa ni Raul,Baaada ya kumpata Raul hakuwa tena na haja ya kuwatafuta majambazi.yeye na mke wake Hajrath walifurahi mno.
SAFARI yao iliishia hapo na hawakutaka kubaki tena katika nchi hiyo baada ya siku mbili walitafuta ndege ikawarudisha nchini India.
Waliendelea kumlea Raul maisha ya kishua mno,Chumba chake kilikuwa kikubwa sana na walimpenda Raul,Siku zote Hajrath alikuwa ni mwenye hofu na alijua Mumewe atakuja kujua ukweli.

****
Kanisa zima lilikuwa kimnya wakimsikiliza Mchungaji Alphonce Kipate,akiwa mbele ameshika Biblia akifungisha ndoa ya Adrian na Jaqlin.WAWILI hao walikuwa wenye furaha na kuzidi kuwa kivutio, kila mtu aliwaonea wivu kwa jinsi walivyopendezana.
“Naomba ufatishe maneno machache kama agano,Mimi Jaqlin Mshana”
“Mimi Jaqlin Mshana”
“Nimekubali kuolewa na Bwana Adrian Mwangenya”
“Nimekubali kuolewa na Bwana Adrian Mwangenya”
“Kwa pete hii,awe wangu mpaka pale kifo kitakapo tutenganisha.kwenye shida na raha,tabu na mateso kwa dhiki na faraja”
Jaqlin alifatisha maneno ya Mchungaji Alphonce na Pete ikaletwa.Alimtizama Adrian na kuchukua mkono wake wa kushoto na kuweka pete kidoleni,Kelele zilizidi mara tatu, kamera zilimulika na sasa ilibakia zamu ya Adrian Mwangenya.
Alifuatisha maneno ya Mchungaji na kuweka pete kidoleni kwa Jaqlin.
“Nyie sasa ni mwili mmoja,Ni mke na Mume ndoa yenu naibariki kwa jina la baba la mwana nala roho mtakatifu Ameen”
Kanisa liligubikwa na fujo za matarumbeta.
Ndoa ikawa imefumgwa.Jovvana japokuwa alikuwa mdogo lakini alielewa ni kitendo gani kinaendelea, hata yeye alikuwepo kanisani muda wote alikuwa akipiga makofi.
Walitoka taratibu mpaka nje baada ya ibada kuisha na kuingia ndani ya Limo na safari ya kwenda kupiga picha za kumbukumbu kuanza.
“Nimesahau kukwambia,umependeza mno Mke wangu”
“Hata wewe Mume wangu”
“wewe ni mzuri sana,umebadilika kidogo pale kanisani nigome niseme sio wewe”
“Ha ha ha ha ha ha acha vituko mume wangu”
Gari zilizidi kuendelea mpaka Mikocheni kwa ajili ya picha,umati wa watu ulikuwa teyari umefika uwanja wa mpira wa taifa,harusi hiyo ilitingisha jiji sio mchezo,uwanja wa mpira ulikodiwa kwa ajili ya harusi, jambo ambalo halikuwahi kutokea Jijini Dar es salaam.
Majira ya saa moja jioni Limo zikawa zimewafikisha maharusi Uwanjani,Ndani ya gari muda wote walikuwa wakinyonyana midomo yao wakipigana madenda.
“Usishuke lav,una lip stick mdomoni ngoja nikupanguse”
Jaqlin alimpangusa Adrian mdomoni kisha kujiweka sawa.
Milango ya Limo ilifunguliwa kisha bwana na bibi harusi waliteremka ndani ya gari mpaka juu kabisa ya uwanja.uliopambwa vizuri, watu wote walisimama na kuanza kuwapigia makofi,kilichowashangaza watu ni baada ya Adrian na Jaqlin kuanza kucheza kwaito huku wakiingia kwa staili sawa.
Jambo hilo lilisababisha waalikwa wasimame na kuungana nao,walikuwa wamechangamka.

Babra alikuwa kwenye viti vya nyuma alishuhudia yanayoendelea na alitamani kwenda lakini alisubiri,kazi yake ilikuwa ni kumpeleka Jaqlin kwa Maxmilian.Alivutiwa sana na Adrian jinsi alivyopanda hewani na mwenye kifua kilichotanuka na rangi yake ya maji ya kunde,alimuangalia kwa macho ya matamanio,alitamani yeye ndiye awe Jaqlin.
Mc maarufu Bakari Jongo ndiye alikuwa na kipaza sauti akizidi kuongea kisha baadaye kumkaribisha Mbunge wa Afrika Mashariki aweze kuongea machache,uwanja ulikaa kimnya.
“Kabla ya yote napenda kumpongeza Mdogo wangu au rafiki yangu Adrian kwa hatua aliyofikia.Nimeudhulia harusi nyingi tofauti ndani na nje ya nchi sijawahi kuona harusi kama hii,kwanza alikuwa ni mwenye furaha,leo nilitakiwa niwepo Adis Ababa kwenye mkutano lakini sikutaka kuwahi,nilitaka nishuhudie hii harusi,kwa hiyo basi ninashukuru nimeiona na ninaondoka leo usiku,napenda kutoa shilingi milioni ishirini,sijui niseme ni yanini lakini naomba mbele yenu niandike hundi hiyo”
Mbunge wa Afrika Mashariki Abasi Kibasile aliingiza mkono ndani ya koti na kutoa cheki, hapo hapo aliandika kiasi cha shilingi milioni Ishirini na kumkabidhi Adrian kisha kuondoka zake.
Mzee Mmoja wa kihaya nayeye alikuwepo na alitaka kuonesha uwezo, alisimama na kuchukua kipaza sauti.
“Actually,Sisi wahaya hatuna Rongo rongo buana Adrian mimi naandika hundi ya Mirioni Thelathini na pia nakuzawadia bonge la gari hiro sijui utampa house gal wako ni gari ndogo Landcruiser Vx ya kuwendea majanini,Mimi pia napenda kumuita ndugu Rubashorwa aje nayeye hapa aripe niliyosema”
Mzee Kibumu hakuwa na masihala alitoka nje na kuandika hundi,kisha Mzee Rubashorwa kusimama.
Ulikuwa kama mchezo kila mtu alianza kuonesha mabavu na kwa hesabu za haraka ilipatikana kiasi cha shilingi millioni Mia saba huku wengine wakiwa wamehaidi.
Ilivyofika saa nne ya usiku hawakuyaamini macho yao baada ya kuona ndege ndogo inatua nje kwenye lami jambo ambalo lilizidi kuamsha hisia za watu,Mzee Mwangenya pamoja na Wazazi wa Jaqlin na baadhi ya ndugu wa karibu ndiyo walioingia ndani ya Ndege pamoja na Adrian,Jaqlin na Jovvana.

Ndege ilitembea kwenye lami kisha kupaa angani,pombe ziliendelea kunywewa ndani ya ndege,rubani alikuwa ana kazi ya kuizungusha ndege hiyo hewani.
Kweli harusi hiyo mpaka dakika hiyo iliweka heshima kubwa haikutingisha Dar es salaam peke yake.Ilitingisha Tanzania nzima kwa ujumla.Ndege ilizunguka hewani masaa manne na kurudi uwanjani.
Ndani ya ndege walibaki Adrian,Jaqlin pamoja na Jovvana kisha ndege kupaa tena hewani.
Jambo hilo lilimshtua sana Jaqlin hakuelewa ni wapi ndege hiyo inapopelekwa na Rubani.
“Baba Jovvana”
“Naam”
“Wapi tunaenda?”
“Honeymoon”
“Ndiyo. ni wapi?”
“China,Hongkong”
“Mhhhh”
“Jovvana fumba macho”
Jaqlin alimuomba Mwanaye naye akatii.
Hakuna kilichofuata hapo zaidi ya Jaqlin kumsogelea Adrian karibu na kuanza kulana denda huku ndege ikiwa hewani. Walivyofika Zanzibar Airport ndege ilitua na kupanda ndege kubwa.safari ilikuwa imepangwa na Adrian na kila kitu kwenda sawa.
Saa tano kasorobo juu ya alama Asubuhi ndege ya shirika la kichina lilikanyaga ardhi ya Hongkok na kusimama,Wote walishusha mizigo na kuanza kushusha ngazi.
Majengo marefu kwenda juu yalimshangaza Jaqlin sababu ndiyo ilikuwa kwa mara ya kwanza kufika nchi hiyo katika maisha yake.
“Baby huku ulishawahi kufika?”
“Ndio nilipita huku kote,nilishawahi kuishi Bangkok,Hongkok nimeishi, ni muda sana hata mji umebadilika kiasi chake”
“Sikuwezi,sasa huku ulikuwa unafanya nini?”
“kutafuta Maisha,pia ile kampuni yangu niliingia mkataba na mzee mmoja wa kichina,nikaja naye mpaka huku kumalizana”
Mazungumzo yao yalifanyika wakiwa wanatoka nje ya uwanja.
“Dad mwone Jet lii,Dad Jack chanie”
Sinema za kichina zilimfanya Jovvana apige kelele baada ya kuwaona watu wafupi wenye macho madogo na kudhani ni wacheza filamu aliowazoea kuwaona kwenye televisheni.

Jaqlin na Adrian walifurahi na kutafuta Taxi iliyowapeleka mpaka kwenye hotel kubwa na ndefu kwenda juu yenye kila kitu ndani yake.
Vyakula vya China! kama Chura,Ubongo wa sisimizi na panya vilimfanya Jaqlin ahisi kichefuchefu kikali.
“Sasa ndiyo nini? Kula mama”
“Adrian wallahi,leo sikupi unyumba ukila hao wadudu”
“Ha ha ha ha ha haha mbona watamu hawa,onja kidogo”
“Staki staki staki Adrian kula na mwanao”
Wachina walikuwa ndani ya mgahawa huo na wengi walikuwa wanagombania Vyura na nyoka wakati mwingine hata kudiriki kupigana misumbwi, chakula hiko ndiyo kilikuwa kikubwa kwao.
Walihama mgahawa huo sababu Jaqlin hakutaka kabisa kuendelea kubaki,
walitafuta tambi na kuanza kula.
Usiku ulivyofika walirudi Hotelini na kumlaza Jovvana.
“Adrian nikwambie kitu?”
“Niambie Mke”
“Nakupenda”
“Namimi na……Mhhhhh”
Adrian hakuweza kumalizia maneno yake,Mdomo wake ulikuwa ukinyonywa na hapo hapo kutupana kitandani puu.Na kuanza kuvuana nguo zao na kubakia kama walivyozaliwa.Walikuwa ni wenye furaha sana na kila mtu alimuona mwenzake ni mpya.
Walibiringizana kitandani mara Jaqlin apande juu mara Adrian apande juu ili mradi Vurugu,kila mtu alikuwa katika heka heka za kutaka kufanya mchezo huo wa kikubwa unaopendwa sana duniani.
Maziwa ya Jaqlin sasa yalikuwa yakinyonywa vizuri na huku mkono wa Adrian ukiwa chini ya ikulu.huku wakiendelea kucheza na ndimi zao.Adrian alitoa ulimi wake ndani ya mdomo wa jaqlin na kuanza kunyonya kitovu mpaka kushuka chini chumvini kisha kuanza kudeki bahari.

 Siku zote Adrian alikuwa hodari kitandani na hakuwahi kuharibu mechi tangu aanze kuujua mwili wa mwanamke,kwa hesabu za harakaharaka alishalala na wanawake sio chini ya mia moja na saba,achilia mbali alivyokuwa Afrika kusini na nchi mbalimbali kama Dubai na Italy.
Hii ilimfanya awe kungwa.umalaya wake ukawa ndiyo unampa uzoefu mwingi wa mchezo huo wa kikubwa unaopendwa duniani kote.
Miguu ya Jaqlin ilikuwa imepanuliwa na ameishika kwa mikono yake huku akiwa anadeki bahari taratibu mno tena bila papala,alichukua mkono wake mmoja na kuupitisha mpaka kwenye chuchu na kuanza kuitomasa kwa juu.
Jaqlin alijihisi raha za ajabu mno!kazi yake ilikuwa ni kutibua kitanda akiyashika mashuka huku na kule na mdomo wake kuuacha wazi,zilikuwa ni raha ambazo alihisi yupo juu ya dunia na vitu vingine anaviona kwa chini,kifupi alijiona yupo angani ana mabawa,hakujua afanye nini zaidi ya kuchukua mkono wake mmoja na kuanza kukikandamiza kichwa cha Adrian ndani kabisa ya chachandu yake kutokana na vitu alivyoanza kuvisikia vinaanza kutoka,Miguno ilizidi mara mia moja.

Adrian hakujali,alishakuwa dokta na alielewa hizo ni dalili za ugonjwa gani siku zote kwa mwanamke na ndiyo maana alizidisha kupiga kasia akizidi kulamba chachandu huku wakati mwingine akijaribu kutumia vidole,hapo ndipo Jaqlin alipoanza kupiga kelele nyingi na kuanza kutetemeka kama aliyepigwa shoti na kuibana miguu yake,Adrian aliiwahi kiufundi nayeye kumpenyeza Nyoka wake shimoni aliyekuwa mrefu na mnene.
Siku hiyo Adrian aliita ‘afe mtu afe m-masai shuka libaki’
na ndiyo maana alitaka kufanya kufuru, alielewa aliacha gumzo gani huko Tanzania na ndiyo alitaka afanye historia mpaka kwa Jaqlin.
Adrian alimchezesha nyoka wake ndani ya shimo kila kona na alimuweka Jaqlin mkao ambao nyoka wake atakuwa anauwezo wa kufika mpaka mwisho na kufika ukingoni,aliipanua miguu ya Jaqlin na kuiweka mabegani vizuri huku mguu wa kulia ukiwa Magharibi na Mwingine kaskazini!Alivyoona hiyo haitoshi alimuweka Mbuzi kagoma na kumweka vizuri karibu na pembe ya ukuta na kuendeleza mashambulizi.
Jaqlin alitoa machozi ya raha,hakuamini. Hapo alifunga goli la pili na la tatu baada ya muda mfupi.Adrian alikuwa bado anapeleka majeshi majeshi,Pumzi alikuwa nazo za kutosha.
Majasho yalimtoka lakini hakutaka kutoa mapumziko.Na hata alivyoshinda bao la kwanza Mpira haukuwekwa kati bali uliendelea kuchezeka ikawa ‘two in one’.
Jaqlin nayeye alijituma alishaona mechi hiyo ina upinzani kiasi gani, ilibidi apashe ndani kwa ndani.Adrian hapo alimchomoa nyoka wake katikati ya mchezo na kuanza kudeki tena bahari.
Wakawa kama wanaanza upya.Adrian alivyotupa macho pembeni aliona mlango wa chooni upo wazi na kuona sink la kuogelea,hapo ndipo alipomuingiza nyoka wake ndani ya shimo na kumbeba Jaqlin huku wakiwa wanapigana denda.
Adrian alikuwa ana stamina asingekuwa nayo asingethubutu kufanya zoezi hilo habadani.Waliingia ndani ya maji na mambo kuendelea,Mambo yaliyoendelea humo yaliogopesha kwa wanandoa hawa.
Siku hiyo waliitumia sawasawia,walikumbuka mengi waliyopitia na shida zote kuzitupa chini kifupi walibanjuka!
Mpaka mechi inaisha saa tisa ya usiku Jaqlin alikuwa hoi bin taaban hata mguu alishindwa kuuinua,tangu amjue Adrian katika michezo ya kitandani hakuwahi kufikisha round kumi na mbili tena kwa muda mfupi, ilikuwa ni maajabu,hakuweza kudhani kama kuna kitu kama hiko kitakuja kutokea,Alibakia akimtizama Adrian aliyekuwa ameyafumba macho yake anatafuta usingizi.
“Baby,naona leo ulifanya komoa,uliambiwa nakufa kesho nini?”
“Vipi unataka tena?”
“Sasa unataka kuniua”
“Nakutania,hata ivyo nimechoka,kiuno kinauma kesho unakazi ya kukikanda Mke wangu kipenzi”
“Nime enjoy sana Darling,sikuachi naomba popote unapoenda tuwe wote”
“Kukikucha inabidi tusafiri mpaka Beijing tukapige pige picha,tukatembee kule”
“Huku tutakaa kwa muda gani?”
“Mimi nakusikiliza wewe hapo”
“Wiki tatu zitatutosha”
“Kweli?”
“Ndio”
“Mbona ndogo?”
“Si unajua tunatakiwa tuwahi kutafuta pesa,pesa tuliyofanyia harusi inabidi irudi”
“Mhh mke wangu nawewe umezidi sasa upare”
“Ha ha ha ha ha ha ha,basi tulale maana umenichosha”
Wote walijifunika na kulala fofofo usingizi mzito sana, Adrian akawa amemkumbatia Jaqlin kwa nyuma wamejifunika na shuka.
***
Hapakuwa na jinsi ya kuzuia hasira za mzee Ahsan Abrahaman siku hiyo,alikasirika mno na kuwaza kuua.Majibu ya DNA kutoka kwa daktari yalimfanya apandwe na jazba.Raul aliumwa ghafla na ilitakiwa damu kutokana na kupungukiwa.Yeye alijitolea na kuambiwa damu haziendani za DNA, ivyo isingewekana kuingiziwa Raul,hapo ndipo alipotaka apimwe DNA, alichanganyikiwa alipoambiwa kuwa Raul na damu yake ni vitu viwili tofauti.
“Dokta una uhakika umepima vizuri damu?”
“Ndio na kinachotakiwa ni damu ya haraka mtoto atafariki”
“Sawa”
Mzee Ahsan alitoka hospitalini haraka na kuingia ndani ya gari lake,Mishipa ya shingo ilimkakamaa kupita kiasi na alitaka kumuuwa Mke wake Hajrath kisha yeye ajiue kutokana na fedhea,mamilioni ya pesa aliyotumia kisa Raul ndiyo ilimchanganya.
Kitu kingine alichotaka kujua ni nani aliyekuwa anafanya mapenzi na mke wake.
Alifika haraka na kuingia chumbani kwake bila kuwasemesha dada zake seblen, alifungua droo na kutoa bastola yake.
Alimsikia vizuri sana mke wake akiwa anaoga bafuni na kumsubiri.
“Hajrath!”
Mzee Ahsan Alimuita mke wake huku akilia machozi ya hasira.
“Abee Mume wangu”
“Kaokoe maisha ya mtoto anaumwa mtafute baba yake sasa hivi kwenye simu ili ajue kabla sijakuuwa”
Hajrath alishtuka na mapigo yake ya moyo kumwenda kasi,siri ilishavuja na alichotakiwa hapo ni kuongea ukweli.

Hakuwahi kumuona mume wake akiwa katika hali hiyo tena kashika bastola,alidondoka chini kwa magoti akilia machozi.
“Usilie Hajrath,mpigie Mwanaharamu wako simu umwambie mtoto wake anaumwa,umeniaibisha vya kutosha kwa uliyonifanyia hustaili kuishi,MAKE A CALL HAJRATH”
Mzee Ahsan akawa amesimama na kumkabidhi Hajrath simu, nia yake ilikuwa baada ya maongezi hayo amuuwe mke wake kwa kumpiga risasi kisha nayeye ajiue.
Kulia kwa Hajrath kulimchelewesha.
Ndani kilijaa kilio na kufanya dada zake wasogee mlangoni kusikiliza nini kilifanya kaka yao apige kelele.

Hajrath bila kuficha alianza kuelezea kila kitu jinsi alivyokuwa akiteswa na wifi zake mpaka alipochukua uamuzi wa Kwenda kwa Roshban na kumuiba mtoto hospitali ya Apolo,aliongea huku akiwa amepiga magoti sakafuni ameishika miguu ya muwe wake.
“Mume wangu nilifanya hivi ili kukulindia heshima yako pia na yangu,nilichoka na manyanyaso ya dada zako,walikuwa wakiniangalia kama kinyesi na ndiyo maana nikafanya i….vyo sikuwahi kumvulia mwanume yoyote nguo yangu,nakuheshimu mume wangu,nakupenda na unalijua hilo..kama kuniua niue tu”
Hajrath aliongea huku akibubujikwa na machozi. kupiga magoti kwa mwanamke wa Kihindi huku akilia kilimaanisha sana.
Machozi ya Hajrath yakawa yamebadili maamuzi ya Mzee Ahsan,ki ukweli alimpenda sana mke wake na alijihisi sio kitu bila Hajrath hapo ndipo alipomuinua na kumkumbatia.
“Nimekusamehe Mke wangu,ila naomba hili jambo liwe kama lilivyo na Raul atabaki kuwa mtoto wetu,nitampenda”
“Nakupenda Mume wangu”
Wote walifutana machozi na kutoka nje haraka haraka wakirudi hospitali ili kumtafuta mtu atakayeweza kumtolea damu na kumpa Raul.Pesa iliongea na haraka mtu akapatikana, dakika hiyo hiyo Raul akawa amepatiwa damu na hali yake kuendelea kama kawaida.Mzee Ahsan alimpenda kama mwanaye wa kumzaa hiyo ikabaki kuwa siri ya watu watatu,Roshban,Mzee Ahsan na Hajrath.

****
Maisha katika jiji la Beijing yaliendelea vizuri na walizunguka kila duka la nguo,kila walichopenda walichukua hususani nguo,walienda kwenye mapiramidi mbalimbali wakiwa na Jovvana.Fungate lilikuwa tamu sana.
“Hii moka lazima nimpelekee mzee”
“Mbona ndefu kwa mbele?”
“Ndiyo anazopenda”
“Lakini hii imezidi khaa,kama ndizi,angalia ilivyopanda juu atakuwa kama jokeri,usimfanye mkwe wangu awe kituko mimi nimependekeza hii hapa ndiyo umnunulie”
“Wee nawe,aya narudisha”
“Baby hili gauni vipi?”
“Wala sio zuri bayaaaaaa”
“Ha ha ha ha ha ndiyo unalipa?”
“Sio nalipa nakwambia ukweli angalia lilivyo kaaa kaa kama kipepeo,yaani ukivaa utatembea mwenyewe,huwezi kutembea namimi,bora gauni hilo hapo ndiyo zuri,embu liangalie,yaani ukilivaa hilo,wanaume watakusumbua na ndiyo hapo nitakufa na mtu,kwanza nataka kununua bastola”
“Heeee yamekuwa hayo,kisa nini?”
“Self defence,marafiki zangu wote wana bastola,mimi ndiyo sina,nikirudi tu namimi nakuwa nayo”
“Mimi sikushauri,na hizo hasira si utakuja kuniulia ndani?”
Maongezi hayo yalifanyika ndani ya duka kubwa la nguo ndani ya jiji la Beijing ndani ya mji wa Importa ndani ya maduka ya gorofa ya Yen juan mchina tajiri aliyewekeza magorofa.
Walivyotoka hapo na kufanya malipo waliingia ndani ya duka lingine la dhahabu tupu kama mikufu,hereni na pete.Kila mtu alikuwa akichagua anachopenda.
“Hii cheni namnunulia Jovvana”
Adrian alimwambia Jaqlin.
“Mhh mhh.sasa unaanza kumdekeza mtoto anaanzaje kuvaa dhahabu akiwa mtoto?”
“Mwache avae”
“Huyo mtoto unavyompenda utafanya awe mjinga,maana kila kitu baba,kila kitu baba,malezi mabovu hayo,nikimchapa unasema namtetea”
“Embu wacha maneno,Mwache Mwanangu avae bling bling,akifika miaka kumi na nane hivi,asitishike na wanaume na asiongopewe,awe ana gari lake,kifupi nataka wanaume wamuogope”
“Unajidanganya hayo mambo ya kizamani,kwani kipindi wewe….”
“Basi basi basi yaishe”
“Nitaanza mimi”
Wote walikuwa wenye furaha na kutoka ndani ya duka la dhahabu.
Hapo walichukua cheni na pete za dhahabu.Walichukua ndege mpaka Hongkok na kurudi.
Kesho yake ikawa ivyo ivyo mpaka inakatika wiki moja na nusu wakawa wamekinai na kuanza kujiandaa kurudi Tanzania.
Lakini walipanga kwanza wafikie JJ HOTEL wakae tena siku tatu ndiyo warudi Dar es salaam ili waanze shughuli za kujenga taifa.
“Hii mizigo si tutachajiwa itazidi mzani maana ni mingi sio mchezo”
“Itabidi sasa unataka tuiache?usisahau kitu hata kimoja Mama Jovvana,tiketi nishapata ila ndege ya kuunga mpaka Dubai hapo tutachukua nyingine”
“Mimi sina tabu ilimradi tufike,safari saa ngapi?”
“Kesho saa tano usiku”
“Sawa Darling”
Mipango ya safari ilianza siku hiyo, kila kitu kilivyowekwa sawa waliiaga nchi ya china wakiiburudisha miili yao usiku na kulivyokucha,walimalizia shopping ya mwisho.Na ilivyofika saa nne na nusu walikuwa teyari wamefika Hongkok uwanja wa ndege.

****
Saa mbili ya usiku ndipo QATAR airways ilipokanyaga ardhi ya Songwe Mkoani Mbeya na hapo ndipo ulikuwa mwisho wa safari yao.Jovvana alikuwa amelala usingizi,walisafiri masaa mengi,kubadili ndege ndipo kuliwachosha.Walishusha mizigo yao.
Kama waliichawia midomo yao kwani walichajiwa pesa kwa ajili ya mizigo kuzidi mzani.
Walisukuma matoroli mpaka nje ya uwanja ambapo walikuta baadhi ya wafanyakazi wa hotel wamekuja kuwapokea sababu walijua ujio wao.
Walionesha furaha sana, kisha kuingia mpaka ndani ya Costa ambayo ubavuni iliandikwa JJ HOTEL iliyotumika kuwapokea wageni kutokea nchi mbalimbali.
Baada ya masaa matatu walifika katika hotel na kuingia ndani ya chumba chao maalumu ambacho huwa hakiguswi na mtu yoyote Yule.
“Uuuuuf nimechoka,tushukuru tumefika salama,twende tukaoge ili tulale”
Waliingia bafuni na kuoga kisha kujitupa kitandani,Jovvana akiwa tayari amelala.

Asubuhi kulivyokucha Adrian akawa wa kwanza kuamka na kushuka ngazi mpaka kaunta ili kujua mahesabu yalivyoenda.
“Hallooo,am Babra”
Adrian aligeuka na kumtizama mwanamke mrembo aliyekuwa ananukia marashi mazuri ya gharama kisha kupeana mikono.
“Am Adrian”

 Babra alikuwa kama mtu aliyepigwa na ganzi mwilini, kitendo cha kushikana mkono na Adrian kilifanya mapigo yake ya moyo yadunde na damu kumuenda kasi hakuelewa hali kama hiyo imetokeaje.
Alizidi kumtizama Adrian aliyekuwa bize na mahesabu,Mkono mkubwa wa Adrian na kifua kipana kilizidi kumpagawisha, t-shirt iliyombana ndiyo ilikuwa tatizo kwake.
Adrian hakuwa mtu wa mazoezi lakini alikuwa ana kifua kilichotanuka na mwenye urefu mzuri kwenda juu hewani.
Midomo yake myekundu kwa mbali ndio ulikuwa ugonjwa wa Babra na kufanya udenda umtoke,Kweli alimuangalia kwa usongo.
“Dennis tumeishia wapi?”
“Hapa ulikuwa unauliza milioni tano na nusu imekuaje,ndiyo nikawa nakueleza kwamba,pesa nyingine niliwalipa wafanyakazi nyingine ikaingia kwenye bajeti ya mafuta ya magari,nyingine kwenye stock ya vinywaji,ndiyo ikabaki milioni tano na nusu”
“Nipe na risiti zote”
“Sawa”
Risiti zililetwa na kuanza kuzikagua.Adrian alikuwa ni mtu makini na mfuatiliaji katika hotel hiyo.
“Mbona sijaona oda ya Konyagi?”
“Ayaaa! konyagi nimesahau bosi”
“Denisi Denisi,mimi nakufanyia fea,unadhani mama Jovvana akisikia huu uzembe hapa unadhani atakuacha?atakufukuza kazi nadhani umeona wenzako alivyowafanya”
“Naomba usimueleze,leo hii nitanunua”
“Acha uzembe”
Adrian baada ya kumaliza hesabu alipandisha ngazi na kuingia Chumbani kwa Mke wake ambaye alikuwa bafuni anaoga,kwa kuwa alikuwa bado hajaoga nayeye alivua nguo na kuingia bafuni.
“Leo nisugue mgongo Mke wangu”
“Ndio kazi yangu hiyo”
Walicheza michezo mbalimbali ya mahaba bafuni na mwishowe kujikuta wananyonyana midomo yao.Kila mtu alimuona mwenzake mpya siku zote.Adrian alimpenda vibaya mno Jaqlin na kila siku zilivyozidi kwenda alikiri mwenyewe kuwa msichana huyo ni mzuri kuliko wote duniani!

Walivyotoka kuoga wote walishuka ngazi mpaka nje ili wapate kifungua kinywa wakiwa na Jovvana tayari.
Babra alivyowaona aliingiwa na wivu lakini hakutaka kufanya lolote,alichotaka yeye ni apate nafasi ya kuongea na Adrian.
“Hivi hii kazi nitaiweza kweli?mbona huyu mwanaume kaniingia akilini kiasi hiki,lakini sina jinsi lazima niikamilishe hii kazi alafu nimrudie Huyu Mwanaume,ki ukweli ana mvuto,sijui kitandani atakuwaje”
Hayo yalipita kichwani kwa Babra macho yake yakiwa ameyatupa kwa Adrian muda wote akimshangaa kwa matamanio.
Siku zilivyozidi kwenda ndipo sura ya Adrian ilizidi kumwingia akilini na kuzidi kuumia kila alipomuona anaongozana na Mke wake na kushindwa kuvumilia.
Siku hiyo Adrian alikuwa peke yake anaongea na simu, Babra alipiga hatua za taratibu na kumuendea Kisha kumsalimia.
“Adrian vipi?niliambiwa wewe ndiye mmiliki wa hii hoteli?”
“Ndio! mimi na mke wangu ndio wamiliki”
“Woow inapendeza sana,ujue napenda sana kuwaona mkitembea pamoja na mke wako,hata ivyo nilikuwepo kwenye harusi yako,ilikuwa kubwa ilipendeza sana”
“Ahsante,nashukuru sana”
“Vipi lakini biashara ya Hotel ina faida?”
“Ivyo ivyo,unajua ukianza biashara inakubidi ukubali hasara,hata hasara ni sehemu ya biashara pia”
“Mbali na Hotel mna miliki vitu gani vingine?”
“Kuna migahawa, nyumba za wageni na biashara nyingine,naomba niondoke mke wangu ananisubiri nje,baadaye tutaongea”
“Sawa”
Adrian alitembea mpaka ndani ya gari na kuondoka zake akimuacha Babra akimtizama.
Hatua aliyofikia mpaka hapo kidogo ilimpa moyo kwa asilimia Fulani.
Kwa uzuri aliokuwa nao aliamini ni lazima Adrian atanasa kivyovyote vile,alienda mpaka kaunta na kuomba namba za Adrian.
Usiku ulipofika alianza kuchat naye huku wakianza kuchat vitu mbalimbali hususani maisha na biashara.
Babra alijitambulisha kwa Adrian kama muwekezaji na ana viwanda mbalimbali nje na ndani ya nchi, hivyo alikuja Afrika kuwekeza.
“Baby”
“Abee”
“Kuna binti anajaribu kunizoea zoea nashindwa kumuelewa”
“Binti gani?”
“Yule niliyekwambia jana”
“Bado anaendelea?”
“Embu angalia meseji zake,mimi mwenyewe sijui kiingereza vizuri naona ananizingua tu”
“Kwani ni nani? na anataka nini?”
“Anadai yeye ni muwekezaji na amekuja huku kuwekeza”
“Ni raia wa wapi?”
“Sikuumiliza,ila Yule ni Africast,ana mchanganyiko wa mataifa mawili,alafu nimekumbuka kesho naenda kuchukua bastola yangu”
“Kumbe ulikuwa siriazi?”
“Mimi sitanii,leo ndiyo nilimaliza taratibu zao,kesho ndiyo naenda kuchukua”
“Lakini kuwa makini baba na hiyo bastola”
“Mbona unaogopa?”
“Sio naogopa,mimi nakufahamu na hasira zako za ajabu na huo wivu wako,isije ikakutokea puani,Mimi keshokutwa naondoka inabidi Jovvana arudi shule”
Ni Kweli kesho yake asubuhi Adrian alifika Hotelini na bastola ndogo mtu wa kwanza kumuonesha alikuwa ni Jaqlin huku akijisifu.
Haikupita hata siku moja akawa amempiga mfanyakazi wake risasi ya mguu kutokana na kumjibu vibaya mteja tena alimtukana.
“Nilikwambia Baba Jovvana,unaona hasira zako,tunaenda tena kumtibu, hasira hasara,hiyo bastola itakusababishia matatizo”
“Samahani zilikuwa ni hasira,risasi ilifyatuka bahati mbaya sikuwa na nia ya kumdhuru”
“Sasa ungempiga kichwani si yangekuwa mengine,Kuwa makini mume wangu”
Siku mbili walishinda hospitali.polisi walipojaribu kufuatilia Kesi, Jaqlin alitoa rushwa na kesi kufutwa, mambo yakawa shwari, ili kutoa ukali wa kesi hiyo Mfanyakazi aliyepigwa risasi alipandishwa cheo.

Jumatano saa kumi ya jioni Adrian alikuwa uwanjani Songwe anawaaga Jovvana na mke wake kuelekea Dar es salaam siku hiyo.
Jovvana alilia machozi na kugoma katakata kusafiri bila baba yake na hilo lilichukua muda mrefu kumbeleleza.Mtoto huyo wa kike alimpenda sana baba yake kupindukia, ilikuwa vigumu kukaa naye mbali.Ilibidi Adrian ambebe.
“Jovvana”
“Dad! Sitaki kuondoka bila wewe,sitaki mimi labda tubaki wote,sitaki sitaki sitaki sitaki”
“Nisikilize baba anakuja kesho”
“No Dad sitaki nishasema,siwezi kukaa mbali nawewe Dad,napenda uwe karibu nasisi”
“Mama yako yupo mbona?”
“Mimi nakutaka wewe”
Jovvana alilia machozi na hakutaka kutoka mikononi mwa Baba yake,ilikuwa bora nayeye abaki kuliko kuondoka na kumuacha baba yake mbali.
“Sikia Jovvana unatakiwa kurudi shule,mimi nitakuja kesho nimekosa tiketi,nilipenda kusafiri nawewe pamoja na mama yako.Nakupenda Mwanangu nenda na mama”
Ilichukua dakika kumi nzima kumfanya Jovvana atulie na kukubali.
“Dad kesho usipokuja je?”
“Nichape”
“Ndio nitakuchapa”
“Nipe tano”
Jovvana alitabasamu na kupeana tano na baba yake,roho yake iliridhika.
“Baba Jovvana kuwa makini na hiyo silaha”
“usiogope,sasa funguo za BMW zipo ndani ya shati langu jeupe nafikiri,utampa Shabani apeleke gereji,maagizo mengine nitakupa ukifika salama”
Adrian aliiaga familia yake kisha yeye kurudi ndani ya gari.
Hazikupita hata dakika sabini alipokea simu kwa Jaqlin kuwa amefika salama teyari jijini Dar es salaam.
****
Kila kukicha Babra alikuwa ana kazi ya kufikiria ni jinsi gani aweke mitego ya kumnasa Adrian kimapenzi,kuvaa vimini na kupandisha maziwa vyote viligonga mwamba,ilifika kipindi alimpigia Adrian simu usiku waweze kuongea lakini juhudi zake hazikuweza kuzaa matunda.
Adrian sio kwamba hakutegeka bali alimuheshimu Jaqlin na isitoshe aliwakinai wanawake kwani ladha ni ileile,alishaamua kutulia, alimchukulia Babra kama rafiki wa kawaida ivyo hakumuweka akilini hata siku moja.
Siku moja usiku Adrian alisikia mlango wake unagongwa na alivyofungua alimuona Babra nje amevalia nguo ya kulalia huku sidiria ya ndani pamoja na chupi aliyovaa kuonekana.
Adrian alikuwa amevalia boxa na mashine yake ilikuwa imesimama sababu alikuwa ametoka usingizini akawa hajatarajia ugeni wa kike usiku huo ndiyo maana alitoka ghafla.
“Vipi?”
Babra badala ya kuongea alichukua mkono wake na kuuweka juu ya mashine ya Adrian na taratibu kuanza kuichua,alifanya hayo yote sababu alishapewa umbea kuwa Jaqlin hayupo.
“Jieshimu!”
Neno moja tu lilimfanya Babra aogope tena mkono wake ulitupwa mbali na kilichofuata hapo ni kelele ya mlango kubamizwa.
Adhma ya Babra ikawa imegonga Mwamba kwa mara nyingine.
Alirudi chumbani kwake,Usiku aliweweseka na baridi kwa hamu aliyokuwa nayo ilibidi atumie vidole vyake akijiingiza ndani ya ikulu yake huku hisia zake zikiwa mbali,alichukua simu yake na kuanza kuangalia filamu za ngono na kuanza kuvuta hisia akiwa na Adrian kitandani,alihema mwenyewe juu juu mpaka alipofika mshindo.
“Lazima nimpate huyu mwanamme,hata inichukue miaka,anaringia nini?Mimi ni mzuri na hakuna mkate mgumu mbele ya chai tena ya maziwa,atalainika tu”
Mawazo hayo yalimiminika kichwani mwa Babra usiku akijaribu kupanga mikakati ya kumnasa Adrian Mwangenya anayeonekana kuwa kauzu kwake kama dagaa kamba!
“Matajiri mbalimbali kulala namimi kwenyewe mpaka waache madola sembuse huyu vishilingi,hivi anajionaje,au hanisi lakini sio nilimuona kasimamisha na dude lake kubwa kwelikweli inaelekea anajua sana kitandani,wallahi simuachi nitakula naye sahani moja”
Kifupi Babra hakulala, kila akijigeuza anashtuka na kujikuta anamuwaza Adrian.


*******
ENDELEA KUSOMA HADITHI NA SIMULIZI ZA MTUNZI….EMMANUEL F.KWAY(THE STORY MASTER)

0 comments:

Post a Comment

BLOG