Search This Blog

Sunday, May 31, 2020

SLAVE SEX SEHEMU YA 10 MWISHO


SLAVE SEX
MTUNZI….EMMANUEL F.KWAY(THE STORY MASTER)
AGE…(18+)
WatsApp…+255718 862176
SEHEMU YA 10 KATI YA 10
*******

Ingawa bado mawazo yalimtesa na alikuwa na bibi yake pamoja na Rukia lakini hakutaka kuliongelea swala hilo,akachukulia ni kama ndoto tu.

Kazi yao ilikuwa ni kumfariji Bibi yao kila kukicha,wakipata nafasi walifika shambani kusafisha makaburi ya Gloria na Nickson huku wakifanya mawasiliano na Dustan.
“MZEE ANAENDELEA VIZURI TUMETOKA KWENYE CHUMBA CHA UPASUAJI,KABADILISHIWA FIGO.MUNGU NI MWEMA,TUZIDI KUMUOMBEA”
Huo ndio ujumbe aliokuwa anausoma Sonia kwenye simu uliotokea moja kwa Moja Nchini India kwa Dustan, habari hizo zilimfanya bibi huyu aachie tabasamu kwa mara ya kwanza tangu aanze kumuuguza Mume wake.
Lakini kilichokuwa kinamuumiza akili Sonia ni kuhusu Nasra,ambaye hakuwa hewani tangu siku tatu zipite na tangu siku hiyo hakupatikana simuni.
Siku nyingine mbili zikapita hali ikawa hivyohivyo,hapo ndipo akaamua kuweka vocha ya shilingi elfu ishirini ili amtafute Dustan hewani waongee vizuri lakini hata alivyomuuliza Dustan hakupata jibu lililomridhisha.
“Unasema hukumuona tangu juzi?”
“Ndio,aliniaga anaenda hotelini kulala usiku.Lakini tangu siku hiyo sijamuona.Hapa nilipo nipo na maaskari tunamtafuta”
“Anco..mbona sielewi”
“Ndi…tititii”
Simu ilikatika wakiwa bado hawajamaliza maongezi,Sonia akalazimika kuwasha gari mpaka dukani kununua vocha nyingine sababu salio lilikuwa limekwisha tayari.
Akapiga tena simu ili kuridhika na maongezi.
“Anco…..Enheee.Ulikuwa unasema?”
“Tutampata tu,usijali wala nini”
“Okay,utaendelea kunijuza”
Damu nzito kuliko maji,siku hiyo Sonia hakuwa na raha hata kidogo alimfikiria Nasra.Kama lolote lingemkuta huko ughaibuni basi lawama zote zingekuwa juu yake.
Ili kupoteza mawazo akaingia chumbani na kuchukuwa laptop yake,akaweka mziki wa taratibu.Lakini kuna kitu alionekana kukumbuka,alitafuta Modem na kuichomeka ili kuperuzi mtandaoni.Meseji zilikuwa ni nyingi sana,alivyofungua Email yake ndio usiseme.Meseji iliyomuogopesha ni mojawapo iliyoandikwa ‘SEBASTIAN WAYTTE SENT AN IMAGE’na ujumbe huo ulitumwa siku chache nyuma,haraka akafungua.Kidude kikaanza kuzunguka taratibu kutokana na Mtandao kuwa mbovu mkoani,Kilimanharo,Moshi.
Picha ilikuwa inajifungua kwa madoido,Kama kungekuwa kuna kipimo cha kupima mapigo ya moyo kwa wakati huo yangeonesha moyo wa Sonia unadunda mara mia mbili kwa sekunde.
“MUNGU WANGU!”
Sonia akahisi amepigwa na ubaridi kwenye uti wake wa mgongo baada ya kumuona Sebastian yupo na Nasra,wamekumbatiana.Na chini yake kulikuwa kuna ujumbe mzito uliomfanya ahisi kizunguzungu kikali!



****
Aidan Waytte,pamoja na familia nzima walifika Uwanja wa kimataifa Washngton Dc saa nane ya mchana,hali ya hewa ilikuwa shwari kabisa.Ndio maana hata jua lilikuwa linawaka kiasi.Kila mtu siku hiyo alijuwa kuwa mzee huyo tajiri anaingia nchini Marekani sababu msafara mkubwa uliingia uwanja wa ndege kwa mbwembwe zote hata mapikipiki meupe yalikuwepo.Aidan Wayte alipokelewa kama Raisi siku hiyo.Mabenzi ya milango sita yalikuwa yamejipanga karibu na langoni kabisa.Mzee Aidan Waytee alisubiriwa kwa hali na mali,walinzi waliovaa suti nyeusi walishafika mlangoni kumsubiri na kumpokea.
“Welcome back sir”(Karibu tena Mheshimiwa)
Mmoja wa walinzi alimsemesha Mzee Waytte baada ya kutokeza mlangoni akiburuza begi, nyuma yake alifuatia Santiago pamoja na Sebastian,Pendo na Mwanaye wao waliongozana na Mama Sebastian,Olivia.Walipokolewa mizigo yao na kuongozana na walinzi mpaka nje ya lango ambapo wote waliingia ndani ya benzi la katikati,hapohapo msafara ukaondoka.
Mbali na kurudi nchini Marekani lakini Sebastian hakuwa na furaha hata kidogo,alifikiria mara mbilimbili mambo aliyoambiwa na Sonia kuhusu ugonjwa wa Ukimwi,alikumbuka siku aliyokutana na msichana mrembo aliyeitwa Lissa,akafanya naye ngono zembe bila kinga.Hilo ndilo lilimchanganya zaidi ubongo wake.Japokuwa mwili ulikuwa ndani ya gari lakini akili yake haikuwa hapo kabisa, ilisafiri maili nyingi,tena mbali sana.Jinsi alivyouogopa ugonjwa huo hakuelewa angefanya nini endapo angepimwa na kukutwa nao,alihisi siku hiyohiyo angejiua mara moja na kutoweka duniani kabisa,alijikita kwenye mawazo kwa masaa mengi.

Geti kubwa la kisasa lilifunguka lenyewe baada ya namba fulani za siri kubonyezwa, hapo magari yakaingia na kutembea kwa kama maili tatu,ndipo ukaonekana uwanja mkubwa uliopambwa majani yaliokatwa vizuri,pembeni kulikuwa na nyumba kubwa sana yenye ‘round about’ katikati, yote yakazunguka na kusimama.
Hiyo ilitosha kabisa kuelezea kuwa mmiliki wa nyumba hiyo alikuwa na utajiri wa kumwaga.Gari zote zilivyosimama akashuka mlinzi na kufungua mlango,Mzee waytte akakanyaga juu ya kitambaa chekundu.Ilielekea ujio wake ulijulikana ndio maana maandalizi hayo yalifanyika.
“Well be back sir”
Wafanyakazi wa ndani walimsemesha bosi wao lakini Mzee Waytte aliwapita bila ya kuwaangalia usoni,alionekana hayupo kawaida kabisa,hakutaka kuongea na mtu yoyote yule akazama mpaka chumbani kwake na kujitupa kitandani.
“Aidan”
Olivia,mke wake alitokeza chumbani na kumuita.
“Naam”
“Ndiyo nini umekuja huku umewaacha wageni peke yao?”
“Waambie nimechoka,nimepumzika.Wakitaka kulala sawa.Wakitaka kuondoa pia hakuna shaka”
“Sasa inakuwa sio vizuri,ina ma..”
“Nimezungumza kiingereza kilichoeleweka bila shaka umenisikia,mimi siwezi ki Namibia”
Jibu hilo lilimkata Maini Olivia,ilibidi atulie na kwenda seblen ambapo aliwapa kampani Santiago na familia yake,mpaka inafika usiku ndipo walipoagana na kuondoka zao.
***
Katika siku ambayo Sebastian hatoweza kuisahau katika maisha yake ni hiyo,majibu aliyopokea kutoka kwa Dokta Carlos Miguel yalimfanya mapigo yake ya moyo yapige kwa kasi.Alihisi mwili wake una moto na damu yake imeacha kutembea mwilini.
“You are HIV POSITIVE Sebastian”
Kauli hiyo ilijirudia mara mbilimbili masikioni mwake na kupita kichwani mwake kama mwangwi,alitamani jambo hilo liwe ndoto ili ashtuke!lakini mambo yaliyokuwa yanatokea siku hiyo yalikuwa halisi kabisa kwamba ni muathirika wa ugonjwa hatari wa ukimwi,midomo yake ilimcheza akabaki anamuangalia daktari na kudondosha funguo za gari zilizokuwa mkononi mwake.Bado hakutaka kuamini majibu ya dokta Carlos Miguel.
“Do..kta embu embu nipime tena”
“Hayo ndiyo majibu”
“Ebwana nipime tena,inawezekana haya majibu sio yangu”Sebastian akafoka.
Dokta akamsikiliza,japokuwa alikuwa ana uhakika na majibu aliyotoa kwa mgonjwa wake lakini alilazimika kutii amri,ndiyo maana akamtoa Sebastian damu tena kwa mara nyingine na kuingia maabara.
Akiwa kitini siku hiyo alimuomba Mungu wake ikutwe kuwa majibu siyo yake.
“Kama nikikutwa sijaadhirika,leoleo naokoka!”
Hivyo ndivyo Sebastian alivyopanga,ilikuwa ni bora apate ugonjwa mwingine wowote kuliko wa Ukimwi,alijua sana jinsi unavyotesa na kuuwa vibaya.Kilichomshtua ni kiti cha daktari kuvutwa.
Moyo wake ukaanza kupiga tena kwa nguvu,akamuangalia daktari kwa masikitiko na uso wa huruma akizidi kuomba Mungu majibu yawe yamebadilika lakini haikuwa hivyo,majibu yalikuwa ni yaleyale kwamba ni muathirika wa ugonjwa wa Ukimwi.
“Okay thank you”
Sebastian alijibu na kuinuka kitini haraka,akaokota funguo za gari zilizokuwa chini.Akili yake ilionekana kuchanganyikiwa.
Alitembea hatua mbilimbili kama mwehu na kuwagonga watu vikumbo.
“What is wrong with you?”(Una tatizo gani)
Mama mtu mzima aliropoka kwa sauti baada ya kupigwa kikumbo kikali akadondoka juu ya uchafu.
Hata hivyo Sebastina alikuwa amepotelea kwenye moja ya kona za hospitali akachomoka kama mkuki,akaingia ndani ya gari na kuchomeka funguo za gari.Jinsi alivyolitoa gari ilionekana dhahiri ni kama mtu aliyevurugwa.
Ni dhahiri kuwa bado alidhani yupo ndotoni na muda mfupi atashtuka,ugonjwa aliouchukia na kuuogopa sasa anao,jambo ambalo alishindwa kuelewa atalitatua vipi,kama ingekuwa kuna namna ya kutumia pesa na kuamisha ugonjwa huo kwa mtu mwingine basi alikuwa yupo radhi hata atumie mabilioni ya pesa awe maskini kwa kumuibia baba yake lakini ugonjwa huo haukuwa na tiba.
“Noooo,nooooooo”
Sebastian alipiga kelele ndani ya gari na kuupiga usukani kwa nguvu,akiwa katika mwendo wa kasi anaendesha gari kuelekea mji ulioitwa New York.Huko ndipo aliamini kuwa atapata majibu ya ukweli,bado aliendelea kujipa moyo kuwa majibu hayakuwa yake wanataka tu kumpa presha.
Aliendesha gari kwa masaa mengi barabarani kisha kufika St.Theresa clinic,mjini New York.Hapo ndipo alipoweka mguu kati na kuzima gari akashuka mbio mpaka ndani,hospitalini.
Majibu aliyopewa yalikuwa ni yaleyale hayakuweza kubadilika,ukweli ulibaki kwamba Sebastian ameathirika na visuri vya ukimwi,picha ya Sonia ikamjia kichwani.Mambo mengi yakamiminika ndani ya kichwa chake,akakumbuka jinsi alivyomtukana na kumnyanyapaa Marehemu mama yake Sonia kipindi anaumwa,hapo ndipo alipoamini msemo unaoitwa ‘hujafa hujaumbika’.Kichwa chake akakiinamisha chini na kuanza kumwaga machozi,alilia kwa uchungu,maisha yake tayari yalikuwa yana dosari.
“Mr.Sebastian”
Dokta akamuita jina lake lakini Sebastian akaendelea kulia machozi tu,tena alilia kwa sauti.Alijililia mwenyewe, picha ya msiba akiwa amelala juu ya jeneza amekonda kama njiti ya kiberiti ndiyo ilipita kichwani mwake, hakumsikiliza daktari alitoka zake nje,akiwa analia bado.
Hata alivyoingia ndani ya gari kilisika kilio tu,alilia kwa uchungu mno mpaka kamasi zikamtoka.Na katika maisha yake hakuwahi kulia kama siku hiyo.Alimlaumu shetani na alijihisi mkosaji mbele za Mungu, wakati mwingine kuna kitu kilimjia na kumwambia kuwa amtafute Sonia amuombe msamaha,kifupi siku hiyo alikiwazia kifo chake.
***
‘HATA KAMA NIKIFA LEO NAOMBA MSILIE KWA SABABU NI KWA TAMAA ZANGU,NIMEAMUA KUJITOA DUNIANI,SIWEZI KUISHI NA UGONJWA HUU WA UKIMWI.NINA AMINI HII NI KAMA ADHABU KUTOKA KWA MUNGU,NILIKUWA NAWANYANYAAPAA WAGONJWA WA UKIMWI LAKINI SASA NINAO MIMI.NAKUPENDA SANA BABA YANGU,NAKUPENDA MAMA PIA,NIAGIE KWA MAMA MDOGO HERRIETH,NI MIMI MAREHEMU MTARAJIWA SEBASTIAN’
Barua hiyo aliisoma Sebastian mara mbilimbili akiwa anaikunja na kuiweka juu ya meza yake,alidhamiria kujiua na kutoweka duniani mara moja kuliko kubaki duniani wakati aliamini kifo kinachokuja mbele yake kilikuwa cha mateso,alitaka kunywa vidonge hatari vya sumu ya wadudu walao mazao mashambani iliyoitwa Lethal poison.
Kazi ya sumu hiyo ilikuwa ni kukausha damu hapohapo na kufanya mapigo ya moyo yasimame kwa muda wa dakika mbili.
Hivyo ndivyo vidonge alivyokuwa navyo Sebastian mkononi mwake akiwa chumbani kwake analia machozi, pembeni kulikuwa na chupa kubwa ya wisky,alitaka afe upesi kwa kumezea na pombe kali.Mikono yake ilimtetemeka kama mtu mwenye degedege!
“Soniiiiia”Aliropoka kwa hasira.
Hata hivyo alikuwa ana uwoga,kifo hakikuwa kitu cha mchezo sababu hakuna mtu aliyejuwa akifa anaenda wapi, ndiyo maana mpaka dakika hiyo alikuwa anjishauri ni kitu gani akifanye.Hakuelewa kifo kinafanana vipi.Lakini kuna nafsi nyingine ilimsukuma avimeze vidonge vyote.
“One two thr……”
Sebastian alihesabu namba,lakini alivyofika namba tatu mlango wake uligongwa.
“Ngongongo”
“Who is this?”(Nani)
“Open the door”(Fungua mlango)
Hapo ndipo alipoanza kujuta ni kwanini hakumeza vidonge mapema,haraka akavitupa vidonge chini ya uvungu na kuuwendea mlango,akafuta machozi na kunyonga kitasa ili kumfungulia baba yake.
“Sebastian za asubuhi mwanangu”
“Salama baba”
“Mbona macho mekundu?”
“Hakuna kitu”
“Embu niingie chumbani kwako tuongee kidogo”
Mlango ukafunguliwa wote, Mzee Waytte akaingia ndani,kitu cha kwanza macho yake yakatua juu ya karatasi iliyokuwa mezani.Maandishi yaliyoandikwa aliyaona vizuri,hapohapo aliichukuwa karatasi na kuanza kuisoma vizuri.Alivyoangalia chini akaona kidonge kimoja,barua aliyotoka kuisoma na kidonge kimoja kilichokuwa chini ilimfanya ajue ni kitu gani kinaendelea.
“Sebastian”
Baba akamuita mwana kwa unyonge.
“Yes Dad”
“You don’t have to do this,come here Son”(Hutakiwi kufanya hivi,njoo hapa mwanangu)
Hapo ndipo Sebastian alipoanza kulia kama mtoto mdogo wa miaka mitatu juu ya bega la baba yake mzazi.
“Don’t cry Son”(Usilie mwanangu)
Mzee Waytte alim-bembeleza mwanaye na kumfariji kuwa ugonjwa huo una uwezo wa kumfanya mtu aishi miaka mingi duniani na kwamba asiwe na wasiwasi,lakini yeye Sebastian aliendelea kulia kama mjane,maumivu aliyokuwa nayo moyoni yalikuwa ni zaidi ya msiba.Ugonjwa wa Sebastian ukabaki kuwa siri kubwa.
“Sitomwambia mtu mwanangu hata mama yako hatojua,nitatumia pesa zangu hata nusu ya utajiri wangu kuhakikisha unakuwa katika afya nzuri,nakupenda sana mwanangu”
Ni kweli Mzee Waytte alitafuta daktari wa saikolojia na huyo ndiye alikuwa akimpa matumaini Sebastian na hapo ndipo alipoanzishiwa dozi za kumeza ili kuuwa wadudu walioanza kushambulia seli zake za damu.
“Karibia robo tatu hapa Marekani wanaishi na virusi vya ukimwi wengine wamezaliwa nao kwahiyo isikutishe hiyo,nina kuhakikishia utaishi miaka zaidi ya sabini hapa duniani”
Hayo ndiyo yalikuwa maneno kutoka kwa Dokta Nicholus Parker Zagarino kila siku akimfariji Sebastian.
****
Siku moja akiwa katika mgahawa wa Mackdonald anakunywa kahawa huku anaperuzi mitandaoni ghafla ujumbe mfupi ukaingia,alivyofungua aliutizama vizuri.
“Nasra from where?”(Nasra wa wapi)
Akarudisha jibu.
Hapo ndipo alipojibiwa tena ikaambatanishwa na picha ya mwanamke mrembo ambaye alimuacha Tanzania,sura ya Nasra haikuwahi kumtoka na alifurahi zaidi baada ya kugundua yupo nchini India.Hapohapo wakatumiana namba za simu na tabia yao ya kuongea usiku ikarudi tena,kila kukicha Nasra aliweka simu pesa nyingi kupiga simu kutokea nchini India mpaka Marekani.
Hakuwa na habari na babu yake aliyekuwa mgonjwa,swala la kwenda nchini Marekani siku zote kwake lilikuwa ni kama ndoto lilikuwa ni lazima litimie!
“Nataka nije Marekani rafiki yangu”
“Unataka kuja lini?”
“Siku yoyote,nitumie tiketi basi”
“Mh,hiyo itakuwa ngumu kidogo.Lakini wacha nifikirie”
“Fikiria rafiki yangu”
Jambo hilo kila siku alilisisitiza Nasra simuni,alidhamiria kwenda Marekani hata kwa kutoroka ama kuzamia.Hakuna siku aliyojichanganya kama kusema kuwa Sonia ni dada yake wa damu,siku hiyo stori ziliisha usiku,Nasra akafunguka juu ya familia yake.
“Sonia?Sonia yupi?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Sebastian,akiuliza mara mbilimbili.
“Sonia yule uliyekuwa unamkimbiza siku ile pale Supamaket,hivi alikufanya nini?Mnajuana?”
“Ngoja nakupigia mimi,sasa hivi”
Sebastian akakata simu akaamua kupiga yeye ili amuulize vizuri Nasra kila kitu.
“Enheee Nasra,niambie.Ni Sonia yupi?”
Nasra hakuficha,si alitaka kujipendekeza?angefanya nini? Kwahiyo alikuwa yupo radhi kuongea chochote kile mbele ya Sebastian.Hapo ndipo alipopasua jipu kuwa yeye na Sonia ni mtu na dada yake na ndiye aliyefanya mipango ya yeye kuwepo nchini India.
“Dada angu ananipenda sana,alafu hukunijibu swali,mlijuana vipi?”
“Nikutumie tiketi lini?”
Sebastian akabadili mada haraka,kuna akili mpya ilimjia kichwani.
“Siku yoyote tu”
“Inabidi nikutumie na viza sasa”
“Hakuna shaka”
“Sawa usiku mwema”
Siku hiyo Sebastian hakulala,kitu kinachoitwa usingizi kwake kilikuwa adimu kupatikana.Alimfikiria Nasra na alitamani afike hata usiku huohuo.
“Ha!Haa!Haaa!Haaa!Haaaaa!”
Akacheka mwenyewe japokuwa hakuelewa ni kwanini anafanya hivyo.
***
Asubuhi ya siku inayofuata akaamkia Ubalozini ili kutafuta viza ya Nasra.
“Baby upo wapi?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Brenda baada ya kupokea simu yake.
“Vipi kwani?”
Sebastian akajibu kwa swali.
“Nauliza tu,sababu nataka kupita hapo kwenu”
“Sipo nyumbani”
“Upo wapi?”
“Embu acha maswali,unataka nini?”
“Nataka nikuone”
“Ngoja nitakupigia”Sebastian akakata simu.
Kwa kutumia mgongo wa baba yake viza ikatoka baada ya siku tatu,Nasra alishatuma kila kitu chake na alichokuwa anasubiri ni tiketi itumwe kwa njia ya barua pepe yaani email.
“Ndiyo nakutumia sasa hivi.Viza yako utachukuwa ubalozi wa Marekani,hukohuko India,nitakutumia pia booking number ukifika ubalozini uwaoneshe,usimwambie mtu lakini kama unakuja huku”
“Siwezi kumwambia mtu yoyote yule”
“Sawa rafiki yangu”
Siku hiyo Nasra alirukaruka kupita kiasi akiwa hotelini,tiketi yake ilikuwa teyari imetumwa.
Hakuna mtu yoyote aliyekuwa anaelewa mpango wake,ili asishtukiwe akaamua kuhama hotel siku hiyo usiku alivyoagana na Dustan.
Asubuhi ya siku iliyofuata alitafuta bajaji mpaka ubalozi wa Marekani.
Akaingia na kupewa viza yake,hakutaka kupoteza wakati.Akarudi hotelini na kupanga vitu vyake,akakaa mkao wa kuondoka.
Siku iliyofuata saa kumi ya jioni aliwasiri uwanja wa ndege Mumbai na kukwea pipa!
***
Hakuna siku ambayo aliyokuwa na mcheche kama alivyopokea meseji kwenye simu yake kuwa Nasra atafika Washngton DC kesho yake asubuhi sana.Usiku kucha alikuwa akiwaza na kuchambua mambo,alimcheka sana Sonia na aliapia kuwa ni lazima angekufa na ndugu zake wote.
Kitendo cha Nasra kuingia ndani ya kumi na nane zake ndicho kilimfanya ajawe na furaha,kilichomfanya ajawe na furaha zaidi ni baada ya kugundua kuwa ni ndugu yake na Sonia.
“Hapa tutakufa wote,lazima nimtie Nasra.Hahahahaha”
Sebastian alicheka siku hiyo usiku mwenyewe.
Kulivyokucha alikuwa na kazi ya kuchambua nguo zake,akatoa shati kabatini jeupe na suruali ya kitambaa ambayo mara ya mwisho aliivaa kwenye maafali ya binamu yake miaka mitatu iliyopita.Alivyoitia mwilini aliiona imem-bana.
“Kumbe nimenenepa eeeh!Ngoja nile lile jeans la Lacoste na hili shati nikivaa na hizi hereni.Mambo yatakuwa supa”
Sebastian alizungumza mwenyewe na kujaribu nguo mbele ya kioo kikubwa.

Alivyoridhika aliingia bafuni kujimwagia maji,baada ya kila kitu kukamilika.Kazi nyingine ikamjia ya kuchagua ni gari gani alitumie.Wazo alilolipata harakaharaka ni gari aina ya ‘Ferrari’ katika magari aliyoyapenda hilo lilikuwa moja wapo, lilikuwa ni gari la chini tena la kisasa na aliliendesha kwa nadra sana.Hicho ndicho alichokifanya,akanyakua funguo na kushusha ngazi.
“Enhee safari ya wapi?”
Mama alitupa swali,baada ya kumuona mwanaye kaunyuka.
“Kwa washkaji”
“Wapi sasa?”
“Mama,naenda kwa Arnold.Ameniambia nikampe kampani”
“Ndiyo asubuhi yote hii mwanangu?”
“Nitawahi kurudi Mama, nakupenda”
Sebastian akaua mada na kutoka nje,ambapo aliliendea gari aina ya Ferrari,milango yake ilifunguka kwa juu,akazama ndani na kulitia moto,safari ya kwenda uwanja wa ndege ikaanza.
***
“How was the flight?”(Safari ilikuwaje)
Sebastian aliongea kwa Swaga baada ya kumpokea Nasra mizigo yake uwanja wa ndege wakawa wananyoosha kuelekea kwenye maegesho ya magari.
“It was safe”
Nasra bado hakuamini kuwa amefika nchini Marekani,kwake aliamini kuwa anaota ndoto!
“Embu njoo kwanza tupige picha hapa moja”
“Sawa”
Nasra na Sebastian wakakaa mkao wa kupiga picha,wakiwa wamekumbatiana.
Hapohapo Sebastian hakutaka kupoteza muda kwa siri kubwa akaingia kwenye ‘email’ na kuiweka picha waliyopiga na kuanza kuandika ujumbe mzito kwa Sonia!
“HALOO BEAUTIFUL IT'S NICE TO HAVE THIS CONVERSATION WITH YOU AGAIN,YOU THOUGHT I COULD SWALLOW IT ALONE? I HAVE ALSO DONE IT THE OTHER WAY ROUND,I DIDN’T BELIEVE AT FIRST THAT YOU COULD DO SUCH A TERRIBLE THING TO ME BUT FORTUNATELY IT’S TIME FOR REVENGE.
OOOH LOL! I ENTRUSTED YOU ALL MY HEART AND FEELINGS BUT I CAME INTO MY NOTE THAT YOU INFECTED ME WITH HIV/AIDS.HA..HAA..HAAA..HAAA!HAAA!HAAAA!HAAAA! YOU DID WITH ALL YOUR HEART SO I’M ALSO GOING TO DO THIS WITH ALL MY HEART,NOW I’VE NASRA AND HOPE YOU UNDERSTAND WHAT IT MEANS.
I KNOW SHE IS GREEN,BUT TRUST ME I’VE TO GIVE HER AS YOU DID TO ME.I THOUGHT OF DOING SOMETHING ILL MORE THAN THIS TO YOUR FAMILY BUT THIS IS BETTER BECAUSE IT WOULD TOUCH YOU MORE AND MORE,LET ME ASSURE YOU I’M GONNA FUC** HER, I WISH ALSO YOUR MOM WOULD BE ALIVE BY NOW SO THAT I FUC** HER TOO.
THEN YOU TELL ME,WHO WINS?FUC** YOU,MOTHERFUCK**……....(habari mrembo,ni furaha kufanya mazungumzo haya nawewe tena,ulidhani nitameza hili swala mwenyewe namimi nimelifanya hili kwa njia nyingine.Mara ya kwanza sikuamini kuwa utanifanyia jambo kama hilo lakini kwa bahati nzuri ni muda wa kulipa kisasi,mara ya kwanza nilikuamini sana na kukupenda mno.Lakini leo umenipa ukimwi.Hahaha ulifanya kwa moyo mmoja namimi pia nitafanya kwa moyo mmoja.Sasa hivi nina Nasra,natumaini unaelewa nini nina maanisha,naelewa hajui lolote linaloendelea.Ninakuhakikishia kuwa nitampa ugonjwa huu kama ulivyonipa.Nilifikiria kuifanya vibaya familia yako lakini nadhani hii ndiyo njia nzuri na itakugusa sana.Naomba nikuhakikishie kuwa……..)
***
Sonia alipokea ujumbe huo ukiwa na picha juu yake akiwa kitandani,akahisi uchungu ajabu.Ilikuwa ni barua iliyojaa matusi kupita kiasi,katika maisha yake hakuwahi kutukanwa na kuumia moyo kama siku hiyo.
Akahisi amevuliwa nguo zake na yu uchi wa mnyama.Aliumia moyo kwa sababu Mdogo wake Brenda alikuwa tayari ana ukimwi na leo Nasra anaupata pia!


***
Akili yake ilivurugika kwa kiasi cha kutosha,ujumbe aliokuwa anausoma kwenye ‘laptop’ yake ukitokea kwa Sebastian ulimvuruga kupindukia.Aliamini kuwa kila alichokifanya yeye ndiye chanzo.Brenda alipata ukimwi kutoka kwa Sebastian nayeye ndiye aliyemuambukiza kwa kufanya naye ngono akiamini kuwa angemkomesha,Nasra alikuwa mbioni kuupata kupitia Sebastian vilevile.Hakuamini kwamba mambo yangezunguka kiasi hicho,bado aliendelea kudhani yupo ndotoni na angeshtuka muda mfupi,akili yake ilichanganua vitu vingi sana akajiona yupo Mbele za Mungu akihojiwa maswali mengi kisha baadaye kutupwa motoni.Hakuelewa ni kitu gani akifanye kwa wakati huo ili kumuokoa dada yake Nasra.
“Lazima nifanye kitu”
Sonia alizidi kuwaza na kuwazua.Siku hiyo nzima ilipita bila kuweka kitu chochote mdomoni,aliisumbua akili yake na kuichosha juu ya kitu gani akifanye,kisasi alichokuwa amekifanya sasa kilirudi kwenye familia yake,hiyo ndiyo ilimfanya ashindwe kufanya mambo mengine.
Japokuwa hali ya Babu yake Mzee Shayo iliendelea vizuri lakini hakuonesha kuchangamka hata kidogo,alimuwaza Nasra.
****
“Mustapha”
“Naam”
“Kuna kitu ninaomba tuzungumze kidogo”
“Hakuna shida”
Siku hiyo Captain Mustapha alitoka Arusha na kufikia Mkoani Moshi,nia yake ikiwa ni kukaa siku moja kisha aanze safari ya kwenda Dar es salaam arudi kazini.Kichwani kwa Sonia kulipita vitu vingi mno,alijisikia kumwambia Mustapha ukweli juu ya ugonjwa wake hatari wa Ukimwi nia ikiwa apewe ushauri.
Kwa jinsi mambo yalivyotokea ilibidi tu aongee, aliamini kuwa mficha maradhi kifo humuumbua!
“Lakini naomba unitunzie hii siri”
“Hakuna shaka shemeji”
Mustapha na Sonia walikuwa peke yao seblen wanazungumza.
“Nina kuomba usinichukulie vibaya kwa ukweli nitakaokupa”
“Usijali kabisa”
Mustapha alikaa mkao wa kupewa habari hiyo,akasogea karibu ili asikilize kwa makini.
“Griii griiiii”
Simu yake ikaita na ndiyo iliyomfanya akatishe kile anachotaka kuambiwa na Sonia,akapokea na kuiweka sikioni mwake.
“Halloo,niambie Tecla”
“Salama,shikamoo”
“Marahaba,vipi?”
“Kaka naomba nikwambie kitu”
“Nakusikiliza”
“Lakini naomba tuongee ukirudi”
“Ongea tu wala usijali”
“Ni kuhusu Tatu”
“Tatu?kafanya nini?”
“Ana ana virusi vya ukimwi”
“Unasemaaa?”
“Dada Tatu ana virusi vya Ukimwi”
“Nilijua tu umalaya ndiyo umemjaa.sasa…”
“Sio iv…”
“Hapana na umwambie hivi kuanzia leo sio ndugu yangu tena,siwezi kuwa na ndugu mwenye virusi vya Ukimwi…Ndiyo nishasema hivyo.Afe tu mwambie asinipigie simu ataniambukiza”
Maneno aliyokuwa anatamka Mustapha simuni yalimuumiza mno Sonia.Ni kweli ndivyo alivyoamini jamii itakavyomchukulia.
Moyo wake ukazidi kuumia sana.
“Eti Sonia”
“Abeee”
“Mtu anakwambia ana ukimwi utamchukuliaje?Si Malaya huyo? kama huyu.Ni mtoto wa Mjomba wangu,mapepe mapepe sana….yaaani”
Katika watu walioogopa ugonjwa wa Ukimwi na kuutafsiri vibaya ni mwanaume huyu Mustapha.Jinsi alivyoongea kwa hasira ilimfanya mpaka Sonia aogope.
“Msichana mdogo anakuwa Malaya,ningekuwa karibu ningemtandika risasi afe kwasababu gani,atawaambukiza wengine”
Mustapha alizidi kuongea maneno ya kutisha mbele ya Sonia.
“Mpaka nataka kusahau.. ulitaka kuniambia nini Sonia”
“Nimenunua kiwanja sitaki mtu yoyote ajue”
Sonia akabadili mada hakutaka kuongea tena ukweli, maneno ya Mustapha yalimuogopesha mno.
“Ni vizuri sana,inapendeza”
“Hasa hasa mchumba wangu sitaki ajuwe,nataka unipe ushauri nipo sahihi?”
“Kwa maisha ya sasa hivi naona upo sahihi kabisa,Katika mahusiano sio kila kitu mpaka ukiweke wazi”
“Lakini pia moyo wangu unaniambia nimwambie”
“Una muda naye gani huyo Mchumba wako,yaani tangu muanze mahusiano?”
“Mwezi mmoja tu”
“Bado bado kwanza”
Sonia ilibidi ayaongeze maongezi hayo ya uwongo,kuongea kwake ukweli kulimaanisha kumuweka mahala pabaya,bado aliendelea kubaki na siri.
Alimsikitikia sana Mustapha sababu ilikuwa ni lazima nayeye aupate endapo atafanya ngono na Nasra,alitamani aseme ukweli lakini aliogopa mno.
***
Gari ya Dustan ilibidi irudi Dar es salaam,alfajiri na Mapema Sonia alidamka na Mustapha alikuwa yupo macho sababu alihitajika mjini kikazi ndiyo maana akaamka asubuhi na mapema,Sonia nayeye hakutaka kubaki mkoani Kilimanjaro,ilibidi arudi Dar es salaam kufikiria ni namna gani afanye ili amnusuru mdogo wake Nasra.
“Mama mbaki salama,niliongea na Anco Dustan atapitia Dar es salaam”
Sonia alikuwa ndani ya gari tayari anaagana na Rukia,pembeni alisimama Bibi yake.
“Na Nasra yeye?”
Rukia akatupa swali,alitaka kujua habari za mwanaye.
“Nasra pia hivyo hivyo”Alificha ukweli.
“Bibi kwaheri”
Wakati anamuaga bibi yake akampa mkono na kumfinyangia noti za elfu kumi saba,bibi huyu wa kichaga akazipokea haraka tena kiutalaam na kutabasamu.
“Haya mjukuu wangu mfike salama,barikiwa sana”
Gari likaanza kuondoka taratibu na Mustapha ndiye alikuwa nyuma ya usukani asubuhi hiyo ya saa kumi na moja.

Njiani hawakusumbuliwa japokuwa Mustapha aliendesha gari kwa kasi sana,kila aliposimamishwa alitoa kitambulisho chake cha Jeshi na kuruhusiwa mara moja.Ndani ya masaa matatu wakawa wameingia Segera njia ya panda ya kuelekea Tanga,gari likazungushwa na safari ikaendelea.
“Huyu Malaya Tatu sijui nimfanye nini,sijui nimtandike risasi?”
“Kwanini?”
Mustapha aliongea na kumuangalia Sonia.
“Si ana ukimwi”
Hakuwa anaelewa lolote kuwa aliyekaa naye pia ana ugonjwa wa Ukimwi na maneno aliyokuwa anaongea yalikuwa makali mno,Sonia alikaa kimnya na kushindwa kuchangia mada.
“Hivi kwani kondomu shilingi ngapi?Mpaka unapata ukimwi in….”
Mustapha akazidi kupigilia msumari swala lake,Sonia akaishiwa pozi na mpaka wanafika mataa ya Ubungo bado aliwaza ni kwa namna gani amuokoe mdogo wake Nasra kutoka mikononi mwa Sebastian japokuwa aliamini kuwa wenda amechelewa.
“Unaishi wapi shemeji?”
Mustapha aliuliza baada ya kufika Ubungo mataa saa tisa ya alasiri.Jua lilikuwa kali mno.
“Mikocheni b”
“Sawa,nitakupeleka kisha nitakuachia gari mimi nitaondoka na taxi”
“Hakuna shaka,hata ukiniacha hapa sio mbaya”
“Siwezi,lazima nihakikishe nimekuacha nyumbani kwako”
Taa za kijani zilivyowaka,Mustapha akaliondosha gari na kukunja kushoto.
Walivyofika Mwenge Sonia akawa na kazi ya kumuelekeza,mpaka walipofika.
“Hapa ndiyo kwangu karibu sana”
“Ahsante,nitakuja siku nyingine”
“Hata maji Shemeji?”
“Hapana,usijali”
“Sawa”
Nyumba ya Sonia ilikuwa kubwa na ndiyo maana Mustapha akabaki anaikodolea macho hakuelewa mwanamke huyu anafanya kazi gani,alitamani kuuliza lakini aliamini hilo halikuwa swala lake.
“Siku njema”
“Ahsante”
Sonia alishuka wakabadilishana upande ili aingize gari ndani,ambapo alifunguliwa geti na mlinzi kisha kuingiza gari.
Kutokana na uchovu hakutaka kufanya chochote zaidi ya kupitiliza mpaka ndani na kujitupa kitandani,mawazo ya kifo chake cha kuteseka ndiyo yalianza kupita ndani ya akili yake.Alivyofikiria ukimwi unavyotesa akakosa raha ya maisha.
Alizidi kuwachukia wanaume kupita kiasi hasa alivyowakumbuka walivyomfanyia.
Alimkumbuka Leythan na kuamini ndiye aliyempa Ukimwi, hakujua yupo wapi kwa wakati huo.
“Mh!”
Hakuelewa kwanini aliguna lakini kuna kitu kilimshtua ambacho hakikuwa cha kawaida,ilipita miezi miwili bila kupata hedhi.Kwa utu uzima aliokuwa nao alielewa nini maana yake ingawa hakutaka jambo hilo liwe la kweli.
“Eh Mungu wangu”
Mahesabu aliyopiga harakaharaka kichwani mwake hayakumuingia akilini hata kidogo,alikumbuka mara ya mwisho hotelini alivyobakwa na Mwanajeshi.Hiyo ndiyo ikamfanya achanganyikiwe zaidi na kutamani kukuche.Usiku mzima aliwaza na hakuelewa angefanya nini angeambiwa ana mimba.Japokuwa alichoka sana na safari lakini hakupata usingizi hata kidogo,alisubiri kukuche ili aelekee hospitali.
***
“Tyson”
“Naam Bosi”
“Nipeleke hospitali,kwa kairuki”
Sonia alimkabidhi funguo mlinzi wake ili safari ya kwenda hospitali kuangalia kama ana ujauzito ianze.
Ni kweli alivyofika Hospitali,majibu aliyopokea yalizidi kumuogopesha sana.Alikuwa ana mimba ya miezi miwili tayari,majibu hayo yalizidi kumfanya aingiwe na hasira dhidi ya wanaume licha ya hapo alikionea huruma kiumbe kilichokuwa tumboni mwake.
“Ahsante daktari”
Sonia alisimama na kufungua mlango akatoka nje,macho kwa macho akakutana na mwanaume ambaye hakuwahi kumtoka kichwani.
“Hafuan”
“Alex”
Sonia nayeye akajibu kwa kutaja jina kwa mshangao!
“Vipi,unafanya nini hapa?”
“Nimekuja kupima Malaria,wewe je?”
“Mke wangu kajifungua leo,nimekuja kumuona”
Alex Mwandambo alipigwa na butwaa la waziwazi,uzuri wa Sonia ulimpagawisha siku zote, ndiyo maana kila kukicha alikuwa akimtafuta lakini alishindwa ni wapi aanzie.
“Leo huyu simuachi”
Alex Mwandambo aliwaza kichwani mwake huku akimuangalia Sonia,kuanzia juu mpaka chini akimtathimini.
“Hongera sana,mtoto wangapi huyu?”
“Huyu wa pili”
“Hongera Baba wawili”
Sonia akaweka utani wote wakacheka.
“Unaelekea wapi sasa hivi?”
Alex akauliza.
“Naenda Home”
“Kuna mambo nilikuwa nataka kuongea nawewe”
“Mambo gani?”
“Inabidi tukae kwanza tuongee”
“Sasa hivi?”
“Hata ikiwa sasa hivi sio mbaya”
“Wapi?”
“Popote tu”
“Okay ngoja kidogo,nisubiri”
Sonia akatoka nje na kumwambia Tyson aanze safari ya kwenda nyumbani kwani yeye atarudi usiku.
***
Ilikuwa ni sehemu iliyotulia na yenye kiyoyozi kizuri,hapo ndipo Mr.Alex Mwandambo alipoamua kukaa na Sonia,hakukuwa na maongezi zaidi ya kujisifia jinsi gani alivyokuwa tajiri na sifa zingine alijiongezea.
“Sasa hivi nina malori ya michanga sabini,nina safirisha mafuta nchi tofauti.Juzi kuna lori langu lilipinduka huko Zambia.Nilichanganyikiwa sana.Mpaka nikaenda India kucheki presha”
“Pole”
“Biashara ya magari inalipa sana,nataka kufungua showroom Magomeni nimeongea na mwarabu fulani hivi naona ananizingua.Nilimkopa milioni mia tisa mpaka sasa hivi hajanirudishia,nimemsamehe”
Mr.Alex hakutofautishwa na muhaya siku hiyo,alikuwa akiongea mambo mengine ambayo yalikuwa ya uwongo,nia yake ilikuwa ni kumjaza Sonia kingi.Ndiyo maana akazidi kupiga ‘fix’
“Wacha niende Alex”
“Hapana baki”
“No,inabidi urudi hospitalini ukakae na mkeo”
“Usijali”
Waliendelea kunywa pombe kali mpaka usiku na Sonia alianza kuhisi kizunguzungu kikali ndiyo maana alitaka kuondoka.
“Hafuan,unaenda wapi?”
“Weeee,usinishikeee…Kaa mbali”
Kama kawaida yake akiwa amekunywa pombe anakuwa mkali kama pilipili mbuzi,lakini siku hiyo Alex hakutaka kumuachia ilikuwa ni lazima amvue nguo yake ya ndani afanye naye ngono.Ndiyo maana akamshika akitumia nguvu na kumkokota mpaka ndani ya gari lake viti vya nyuma na kufunga milango.
“Hafuan”
“Niniiiiiii,nimekwaaambiaa niaaache,nina ukimwiiiii ujueeee”
“Sikiliza basi”
“Aleex,mkeo amejifunguaaa sitaki aje kuwa mjaaaane”
Alex hakutaka kusikiliza, Jogoo wake tayari aliwika,maneno aliyosema Sonia aliyasikia lakini alidhani wenda yupo katika hali ya ulevi,ndiyo maana akamkamata kwa nguvu na kumvuta karibu yake akaanza kumlazimisha kumpiga mabusu ya mdomoni.
Mkono wake ukashuka juu ya ikulu ya Sonia.
Kwa kuwa mchezo huo hakuwahi kuufanya siku nyingi ilibidi atulie nayeye akatoa ulimi wake wakaanza kupigana madenda na Mr.Alex Mwandambo,kumaanisha kuwa yupo tayari kwa tendo hilo la kufanya ngono!


****
Sonia hakuweza tena kufanya chochote, ujanja wote ulikuwa mfukoni sehemu za mwili wake zilizokuwa zinatomaswa haikuwa rahisi kuchomoka na hata angekuwa mwanamke aliyekamilika asingeweza kuruka na kuchomoka,ndiyo maana alilegea na macho yake yakawa malaini akawa kama aliyekula kungu na pombe alizokunywa ndiyo kabisa,akabaki anaguna kwa raha huku akiendelea kubadilishana mate na Alex Mwandambo kwa njia ya ndimi ndani ya gari viti vya nyuma.
Hali ilikuwa mbaya kwake akapitisha mkono wake mmoja mpaka juu ya zipu ya Alex na kuanza kuichua koki yake.
Alex nayeye hakuwa mzembe akajibu mapigo kwa kuitoa nguo ya juu ya Sonia kisha akapachua na sidiria akayafakamia maziwa ya mrembo huyu kwa fujo,bado hakuamini kuwa leo hii kamvua mrembo huyo nguo kirahisi kiasi hicho ndiyo maana akafanya mambo harakaharaka ili tendo hilo lisije kusitishwa.Ilikuwa kidogo aichane suruali yake ya kitambaa sababu ilikuwa haitoki, alitamani airarue,mzuka aliokuwa nao haukuwa wa kawaida,akaivua kwa nguvu akabakiwa na Boxa hakuwa na haja ya kuishusha yote akamvuta Sonia karibu na kumtoa nguo ya chini akashusha chupi yake na kuingiza gunzi lake ndani ya mgodi wa Sonia uliokuwa umebana kiasi,hapo ndipo alipoamini kwamba Sonia hatoweza kutoka.
Walipinduana huku na kule wakiwa ndani ya gari wakiiburudisha miili yao,Alex hakuelewa kuwa yupo katika hatari mbaya kuliko siku zote.
“Hafuan…”
Alex aliita akiwa yupo pembeni anatafuta boxa yake baada ya kumaliza kufanya ngono zembe bila kinga na Sonia.
“Abee”
“Nakupenda”
“Mimi pia,lakini na mkeo je?”
“Achana naye,ni mimi nawewe leo”
“Hivi uliniambia leo ndio kajifungua?”
“Ndio”
“Hongera”
Alex akajifanya hajasikia pongezi,akala buyu!
“Alex hongera”
Sonia akarudia.
“Ahsante,nikupeleke kwako?”
“Mkeo anaruhusiwa lini?”
“Nadhani kesho asubuhi”
“Kwahiyo Utakuwa bize na mkeo unalea?”
Lilikuwa ni swali lingine kutoka kwa Sonia.
“Sio sana”
“Sio sana kivipi?”
“Hafuan nisikilize ki…”
“Unanipenda?”
“Ndio,tena sana tu”
“Naomba ukalale kwangu leo”
“Hafuan,hilo halitowezekana”
“Basi usinitafute tena”
Ulikuwa ni mtihani mkubwa sana kwa Alex,hakuwa tayari kulala nje ya nyumba yake ukizingatia mkewe alijifungua siku hiyo.Licha ya kuwa na Sonia lakini bado alimpenda Mke wake Latifah,hakustaili kusalitiwa sababu alikuwa mpole sana.
“Lakini kesho utaniruhusu niwahi kurudi”
“Usijali,washa gari”
Kisasi cha Sonia kilikuwa ni kwa wanaume, kumruhusu Alex kuondoka siku hiyo aliamini angeenda kumuambukiza na mkewe ukimwi vilevile ilikuwa ni lazima azuie swala hilo lisitokee.Alikuwa na hasira sana na ukoo ulioitwa Mwandambo.Baba yake Alex,Mchungaji Patrick ndiye aliyempa Marehemu mama yake ugonjwa wa ukimwi hilo aliliamini na ndiyo maana hakujutia kufanya naye ngono muda mchache ndani ya gari.Tayari alikuwa amekamilisha kitu alichokuwa anaota kukifanya siku zote kumuambukiza Ukimwi Alex,kitendo alichokifanya Sebastian kilizidi kumtia hasira zaidi.
“Huku au kule?”
Alex alifika katika njia mbili kushoto na kulia akashindwa wapi aende sababu hakupafahamu nyumbani kwa Sonia.
“Kwani hupajuai mikocheni b?”
“Napajua”
“Twende sasa”
“Sawa,ngoja nipitie barabara ya coca cola”
Alex akazungusha usukani na kuzidi kunyoosha,Sonia alikuwa kushoto ametulia pombe bado anaihisi kwa mbali kichwani.
Nusu saa baadaye walikuwa tayari wanapita shule ya Academic,kuanzia hapo Sonia ndiye alikuwa anatoa maelekezo.
“Hapo nyoosha mpaka kwenye hilo geti hapo utaingia”
“Lipi hilo hapo mbele linalowaka taa juu?”
Alex akauliza,hakuwa na uhakika na anachosema Sonia.
“Ndiyo”
“Ndio unapoishi au tunaenda kumuona mtu?”
“Ndio kwangu”
“Sawa”
Sekunde chache gari lilikuwa mbele ya geti kubwa linapiga honi,kabla ya kufunguliwa akatokeza askari wa kampuni ya KK security akiwa na mtutu. Hakutaka kufungua geti kwanza sababu gari hilo hakuwahi kuliona, lilikuwa ngeni katika macho yake,akasogea karibu kioo kikashushwa.
“Askari ni mimi”
Sonia ndiye aliyejibu,hapo ndipo askari akarudi getini na kulifungua.
***
Hakutaka Alex arudi nyumbani kwake,alihofia sana kwa maana hiyo alifikiria kuivuruga ndoa hiyo kwa njia moja au nyingine.Hakutaka Latifah aambukizwe ugonjwa huo sababu hakuwa na hatia yoyote ile, isitoshe alikuwa na watoto wadogo tu,ingewezekana kabisa pia watoto hao kuupata vilevile kupitia mama yao.
“Hafuan naomba niende hospitali kumchukuwa mke wangu”
Alex alisema ilivyofika asubuhi.
“Sasa uniacha na nani?”
“Nitarudi”
“Hapana,twende wote”
“Niamini mpenzi”
“Kwani hakuna mtu mwingine wa kumpeleka nyumbani,mpaka wewe.Kwahiyo hunipendi?”
“Nakupenda”
“Basi mtume mtu akamchukuwe mwambie upo bize”
Sonia aliongea huku akilegeza sauti,kumruhusu Alex kurudi nyumbani kulimaanisha kifo cha Latifah ndiyo mana akainuka kidogo na kuchukuwa simu ya Alex na kumkabidhi.
“Piga simu mpenzi”
Sonia akazidi kusisitiza.Alex akamtizama machoni kwanza,bado alikuwa anajifikiria mara mbilimbili hapohapo akaichukuwa simu na kuonekana akitafuta namba fulani na kuweka sikioni baada ya kuipiga.
“Nani Lazaro,ndioo ndiiooo,Nashukuru ahsante.Sasa naomba unisaidie kitu kimoja….Mke wangu anaruhusiwa leo..Ndi ndio naomba ukamchukuwe..Mimi nipo bize kidogo na nipo mbali…..Haina shida ahsante sana..utamwambia hivyo au nitampigia mwenyewe,ayaaa..Samahani kwa kukusumbua asubuhi…okay siku njema”
Alex alihitimisha maongezi na mtu aliyekuwa anaongea naye upande wa pili wa simu.
Kwa Sonia aliyekuwa pembeni hakusikia lakini alielewa kuwa tayari Alex amenasa kwenye mtego na siku hiyo hatoenda kukutana na mke wake.
“Nakupenda baby”
Sonia alimrukia Alex na kumkumbatia.
“Nakupenda pia ndiyo maana nafanya hivi,Hafuan hauna mwanaume?”
“Kwanini umeniuliza?”
“Nataka kujua”
“Sina mwanaume sasa hivi”
“Niambie ukweli”
“Kwanini nikudanganye Alex”
Alex hakuelewa chochote kuhusu Sonia wala hakujua kuwa yupo katika hatari kubwa ya kupata ugonjwa hatari wa ukimwi laiti angejua angetulia na mke wake,tamaa za mwili zilimponza na mpaka wakati huo alikuwa ni baba wa watoto wawili wadogo tayari, Mackline na Jamal.

Alimsogelea Sonia na kuanza kumtomasa, kabla ya kuanza kupasha simu yake ikaanza kuita,alivyoangalia aliona jina la mke wake.Alijua ni lazima angekumbana na maswali mengi mno.
“Mke wangu huyo,naomba unyamaze”
Alex akatoa onyo kabla ya kupokea simu.
“Halloo Latifah”
“Uko wapi Darling?”
Latifah aliuliza kwa sauti ya unyonge.
“Nipo nipo Kibaha,kuna mambo nafatilia ya kibiashara”
“Umemtuma Lazaro anipeleke nyumbani?”
“Ndio,keshafika kwani?”
“Ndio amefika hapa,utarudi saa ngapi nyumbani?”
“Nitarudi mchana”
“Jamal anakusalimia hapa”
“Namsikia hapo analia”
“Kafanana nawewe”
“Baby,baadaye nitakupigia tena”
“Okay Darling nakupenda”
Maskini ya Mungu Latifah hakujua lolote,hakuelewa kuwa mume wake yupo juu kitanda na mwanamke mwingine wapo uchi wa mnyama, kama simu zingekuwa zinasema ukweli basi siku hiyo Latifah angelia sana na kusaga meno,mambo aliyokuwa anafanya Mume wake hayakustaili kabisa.
“Itabidi niondoke mchana”
Alex alisema na kumgeukia Sonia baada ya kukata simu.
“Baby”
“Naomba nielewe Hafuan,inabidi nikamzuge zuge kidogo”
“Sawa”
Mambo yalianza upya wakaanza kupigana mabusu mfululizo na kushikanashikana,kwa sekunde moja tu Sonia akapanda juu ya Alex na kuingiza karoti ndani ya ikulu yake,akawa ananyonga kiuno chake taratibu licha ya kuhisi mwili wake upo mbali lakini alimsikitikia mwanaume huyu anayeenda kufa kwa ukimwi.
Ilikuwa ni lazima ampe gonjwa hilo kama kisasi.Na hilo aliamini tayari limefanikiwa kabisa.Alex hakuwa na habari yoyote ile aliendelea kukikamata vizuri kiuno cha Sonia akihisi raha za ajabu ,hatimaye akafika mshindo na kutulia tuli.
“Naenda kuoga”
“Sawa,tangulia nakuja”
Alex alivyoingia bafuni Sonia akachukuwa simu yake,akahamisha namba za Latifah na kuzisevu kwenye simu yake kisha nayeye kuingia bafuni ambapo huko walipashana tena, wakafanya mambo ya kikubwa!

***
Ilikuwa ni lazima amuokoe Mwanamke mwenzake tena asiyekuwa na hatia kwa njia moja ama nyingine,alijua sana uamuzi anaotaka kuufanya ungemuumiza Mwanamke huyo aliyetoka kujifungua siku chache tu lakini hakujali ilikuwa ni lazima achukuwe maamuzi magumu kama hayo,alivyohakikisha gari ya Alex imetoka nje ya geti yeye alirudi ndani chumbani kwake na kukwapua simu,akazitafuta namba za Latifah na kuziweka sawa,akaipa simu ‘ok’ hapohapo ikaanza kuita lakini haikupokelewa,hakukoma akapiga tena.
“Hallooo”
Upande wa pili wa simu ukapokelewa na kusikika,tena ilikuwa ni sauti ya kike.
“Naongea na Latifah?”
Sonia akauliza kwa shali.
“Ndiyo, nani mwenzangu?”
“Mke mwenzio,kama hutaki potezea”
“Naaaaniii?”
“Mke mwenzako nimekwambia,kwanza pole kwa kudanganywa…Pia hongera kwa kujifungua vilevile.Nachokuomba achana na Alex kwa sababu ana nipenda hapa nina mimba yake,yupo katika taratibu za kunijengea nyumba…”
Upande wa pili ulikuwa kimnya.
“Wewe Malaya unanisikia?”
Sonia akazidi kutoa matusi makali,kwa mbali alisikia Latifah anavuta kamasi ni dhahiri kuwa machozi yalikuwa yanamtoka,Sonia akaona tayari swala lake limefanikiwa,akazidi kulipigilia msumari.
“Naongea nawewe Malaya”
“Da..da hivi unajua kuwa mi..mi ni mwanamke mwenzako?”
“Kwahiyo?Tena Koma wewe,tena ishia hapohapo.Nachokuomba achana na Alex kabla balaa jingine halijakukuta umenielewa kahaba wewe”
Sonia aliongea maneno hayo licha ya kuelewa kuwa yalikuwa yanamchoma Latifah kupita kiasi lakini hakuwa na chaguo lingine ilibidi afanye hivyo ili amuepushe na janga la ukimwi na aliapia kuisambaratisha ndoa hiyo.
“Sa….sa sawaaa”
Latifah alijibu kwa Kwikwi na kukata simu,machozi yalimtoka yakatiririka mashavuni yakapita na kulowanisha kifua chake,akamtizama mtoto wake aliyekuwa mchanga yupo mikononi mwake.
Hakutaka kuamini ametoka kutukanwa na kudhalilishwa kiasi hicho na mwanamke mwenzake tena siku hiyo ya furaha aliyokuwa anamsubiri Alex wafurahi,akashindwa amfanye nini mume wake akabaki analia tu akiwa chumbani.
Alihisi kuumia sana moyo wake,hakustaili kabisa kufanyiwa kitu kama hicho tena kuitwa Malaya.
“Pipiiii piiiiiiiiii”
Honi ya gari ndiyo ilimzindua,mlio wa gari la mume wake aliujua na ndiyo yeye alikuwa anapiga honi aliamini hilo kwa asilimia mia moja,akasikia geti linafunguliwa na muungurumo wa gari kuingia kisha likazimwa,akasikia tena mlango wa gari unafungwa.
Hazikupita hata dakika mbili mlango wa chumbani kwake ukafunguliwa akamuona Mume wake Alex kaingia akiwa anatabasamu,jambo hilo alilitafsiri kama ni unafki.
“Mke wangu hongera sana,foleni iliniweka kidogo.Nilikuwa na Lucas,Kibaha kule anakupa hongera.Embu mtoto nimbebe,hongera tena kwa mara nyingine”
Alex aliongea maneno mengi kwa wakati mmoja tena bila kuulizwa.


****
Hakuna siku aliyoumia mtima kama siku hiyo asubuhi,ilikuwa ni dakika chache tu zilipita tangu atukanwe matusi ya nguoni kutoka kwa mwanamke aliyempigia simu, tangu azaliwe ama kuingia ndani ya ndoa hakuwahi kuitwa Malaya au kahaba sababu hakuwahi kusimama barabarani na kuuza mwili wake hata siku moja,Latifah alikuwa ni mwanamke wa kiislam aliyelelewa katika misingi imara ya dini hiyo, ndiyo maana alikuwa mpole na aliyavumilia mengi ya Alex lakini ya siku hiyo ilizidi kikomo,mambo yalimfika shingoni.
Akashindwa kuongea lolote akabaki analia na kumwangalia Alex anayezidi kumsogelea akiwa anaongea uwongo.
“Latifah,vipi mbona unalia sasa?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Alex akimtizama mke wake.
“Na..hitaji kurudi nyumba..ni kwetu sija..ua”
“Kuna nini mke wangu?”
“Mimi sio mkeo,Alex ni..mekuvumilia mengi lakini hii ni too much.Tafadhali naomba niende”
“Embu embu embu embu,subiri kwanza kuna tatizo gani?”Alex akapata kigugumizi cha ghafla!
“Kamuulize mwanamke unayetaka kumjengea nyumba”
“Latifa…h”
“Niac.h.e”
Latifah hakuwa na utani,alimuweka mtoto wake kitandani na kuingia kabatini akionekana kuchukua nguo zake,hakuwa tayari kubaki nyumbani tena.Aliamini hilo ndilo lilikuwa suluisho,kuendelea kubaki na Alex kulimaanisha kuendelea kutukanwa,aliamini kile anachotaka kukifanya kilikuwa sahihi kabisa.
“Latiafh”
“Naomba niende”
Latifah bado alikazia msimamo wake,maumivu ya uzazi aliyokuwa nayo yalimtoka na alichotaka yeye ni kuondoka tu.
“Na ninaomba niondoke na wanangu”
“Latifah unafika mbali sasa”
“Nimekuachia uhuru ufanye mambo yako,nina Imani utafaidi”
Huo ndiyo ulikuwa ukweli,Latifah alitoka chumbani na kuingia ndani ya chumba cha Mackline mtoto wao mwingine mdogo mwenye umri wa miaka mitano,akamvalisha nguo vizuri akafanya pia hivyo hivyo Kwa mtoto wake mwingine mchanga Jamal.
Jamal aliwekwa mgongoni na Mackline akamshika kwa mbele,akaburuza mabegi yake kutoka nje akiwa analia machozi anaitizama nyumba.
“Latifah”
Alex alibaki mlangoni anamtizama mke wake anatoka nje,alihisi uchungu kumpoteza mke wake.Yote hayo alijua yalifanywa na Sonia ingawa hakuwa na uhakika sana.Geti likafunguliwa na mlinzi Latifah akatoka nje.Hapohapo bila kujifikiria akaingia ndani na kuchukuwa simu yake iliyokuwa kitandani,alitaka kumpigia Sonia na ndicho alichokifanya.
“Hafuan,ndiyo umefanya nini sasa?”
“Kufanya nini kivipi?”
“Nani kakwambia umpigie mke wangu simu?”
Alex aliongea kwa jazba.
“Sasa unamfokea nani?”
“Wewe hapo”
“Sijawahi kufokewa tangu nizaliwe”
“Unanijibu nini wewe?”
“Kama ulivyosikia,mimi nakupenda ndio maana nafanya hivyo.Hivi unadhani mimi sina moyo au?Nimeshindwa kuvumilia ndiyo maana nikapiga simu kwa mkeo”
“Hauna akili kabisa”
“Sawa lakini ndiyo ivyo,kaondoka kwani?”
“Ndiyo”
“Woow!nimefurahi.Naomba unioe mimi”
“Unasema nini?”
“Unanipenda au hunipendi?”
Lilikuwa ni swali lililomfanya Alex ababaike kidogo,ujasiri wa Sonia ulimtisha.Kibiriti alichokuwa anatingisha kilikuwa kina njiti tena zimejaa,Sonia alimjibu kibuli ndiyo maana akashusha sauti akawa mpole,hakutaka kuwakosa wote,Mkewe alishaondoka hakutaka kumpoteza Sonia pia.
“Nakupenda”
“Sasa mbona unanipigia pigia kelele”
“Sorry nilikuwa nina hasira”
“Nakusikiliza Laaziz”
“Bado upo nyumbani?”
“Ndio”
“Nitakuja kuku pick jioni”
“Poa baby”
Sonia alikata simu na kutabasamu,moyo wake ukashuka mapigo kidogo.Kwa kitu alichokifanya aliamini yupo sahihi kabisa sababu hakutaka ukimwi umfikie mwanamke mwenzake asiyekuwa na hatia, Latifah.

Swala la kumuambukiza Ukimwi Alex Mwandambo lilikuwa tayari limetiki,akaenda kwenye kabati na kuvuta draw.Akaanza kusoma majina ya watu aliowaambukiza ukimwi,akaliandika na jina Alex chini yake.Walikuwa ni wanaume wasiopungua hamsini na bado alijisikia kuusambaza kwa wanaume wengine waliokuwa na tamaa.
Kwa uzuri aliokuwa nao aliamini kuwa hakuna mwanaume yoyote yule atakayeweza kupindua kwake.Vitu vingi vilipita kichwani mwake hususani kwa wanaume waliobaki kwenye karatasi iliyoandikwa kwa mwandiko mbovu kabla ya marehemu mama yake kufariki dunia,aliipitia na kuyaona majina mengine.
“Pe..deshee Kway,Patrick Mwa..andambo,Zu..ma….”
Hayo yalikuwa baadhi ya majina ya wanaume aliotakiwa kuwashughulikia ingawa hakuelewa ni kivipi angewapata,akiwa anaendelea kutafakari simu yake iliita namba ilikuwa ngeni,akaitizama kwa makini na kuipokea,akaiweka sikioni.
“Da..da nimekuachi..a uhuru na mume wangu.Nachokuomba uendelee kumtunza bado ninampenda,ahsante”
Sauti hiyo haikuwa ngeni kabisa,simu ilitoka kwa Latifah,alitamani ajibu kitu lakini alishindwa alimuonea huruma sana mwanamke mwenzake, alielewa nini maana ya uchungu wa penzi,sababu alishawahi kusalitiwa na kutamani kujiua.
***
Jiji la Washington D.C lilikuwa katika hekaheka, kila mtu alikuwa na shamrashamra, siku hiyo kulikuwa na sikukuu iliyotambulika kitaifa,japokuwa haikuhalalishwa duniani kote.Ilikuwa ni sikukuu ya mashoga yaani binadamu wenye mahusiano ya jinsia moja.Siku hiyo wanaume mashoga walijipodoa kwelikweli na kuonekana barabarani na mabwana zao.Kwa wazungu sherehe hiyo ilikuwa kawaida kabisa na ndiyo maana ilitambulika kitaifa ikawekwa katika kalenda zao,watu hawakwenda makazini.
“Mpenzi siku hizi sipendi tabia zako”
“Tabia gani hizo?”
“Si ya umalaya wako na siku hizi nasikia una kidemu kipya”
“Achana na hao mademu,wanazusha tu”
“Nakupenda lakini,mimi sipendi ujue”
Kama ungepita dirishani ungedhani waliokuwa ndani ni mwanamke na mwanaume,kumbe haikuwa hivyo.
Sebastian alikuwa amekumbatiwa na mwanaume mwenzake wanafanya mambo ya kishoga,jinsi shoga huyu alivyojiremba na kujilegeza ilimfanya Sebastian apagawe kabisa,Comrad alikuwa shoga kwelikweli tena aliyekubuhu na alikuwa ana sura ya kike.Kila kitu alichokuwa nacho mwilini kilikuwa kama jinsia hiyo lakini isipokuwa maumbile yake kwa ndani.
Kutokana na Sebastian kujiingiza katika makundi ya kihuni akajikuta anadondokea katika tendo hilo la kishenzi lililofanya mpaka Sodoma na gomola kuchomwa moto.Sebastian aliweza kumshughulikia shoga huyu kisawasawa ndiyo maana alipendwa sana.Na jambo hilo lilikuwa siri kubwa mno.
“Leo sikukuku yetu lakini mpenzi”
Comrad alimwambia Sebastian huku akilegeza macho.Alimuita mpenzi kwa sababu alijiona yeye ni mwanamke.
“Naelewa lakini sitokuwepo,wacha tumpuzike”
“Hapana mpenzi wangu,jaamaani aaaaah”
“Usijali,sisi tutaenjoy humu chumbani”
“Sawa tu”
Huo ndiyo mchezo mchafu aliokuwa anafanya Sebastian kwa siri kubwa sana.Alivyomaliza kumshugulikia Comrad kwa mara nyingine alisimama na kwenda mezani,akachukuwa sigara kubwa na kuiwasha akaanza kuvuta.Akavuta moshi wa kwanza,akautolea puani.
“Mpenzi,mimi nakuacha basi”
“Unaenda wapi jamani?”
“Naenda nyumbani mara moja”
“Sawa lakini nitakumisi”
“Hata mimi”
Sebastian akatembea na kubeba funguo zake za gari akafunga mlango na kutoka nje ya Hotel.
“Ametoka nje”
“Anaendesha gari gani?”
“Ramborgin ya silver”
“Sawa”
Yalikuwa ni mazungumzo yaliyotokea kwa Comrad kupitia simu.
“Kwahiyo mtamuuwa au?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Shoga Comrad.
“Wewe tuachie sisi njoo uchukuwe chako”
“Sawa”
***
Sebastian alitoka nje na kuingia ndani ya Ramborgin akaliwasha na kuondoka zake,hakuelewa lolote linaoendelea nyuma yake.Gari aina ya Ford nyeusi ilikuwa nyuma yake inamfuatilia.Japokuwa aliliona gari hilo kupitia ‘site mirror’ za nje lakini hakushughulika nalo.Akafika kwenye moja ya mgahawa wa Mackdonald na kuweka gari nje kisha kuingia.
“Oh Nasra,ulinisubiri eeh?”
“Sio sana,ndiyo nilikuwa namalizia baga yangu hapa.Ulifanikiwa?”
“Kiasi chake,nikurudishe hotelini au?”
“Vyovyote sawa”
“Sasa vipi kuhusu yale maswala,lile ombi langu?”
“Ombi lipi tena?”
“Uwe mpenzi wangu”
“Hilo halitowezakana kwa kweli,nilishakwambia”
“Sasa Kwanini?”
“Hapana,basi tu siwezi”
Nasra hakuwa tayari kuwa na mahusiano na mwanaume huyu Sebastian,hakuelewa kwanini moyo wake ulikuwa ukisita kiasi hicho.Tabia nyingine iliyomkera Nasra ni kitendo cha Sebastian kujiingiza katika maswala ya kuvuta sigara na matumizi ya bangi!
“Au kisa natumia vilevi vikali?”
Sebastian alijishtukia na kutupa swali.
“Hapana hiyo ni starehe kama nyingine tu,siwezi kukuchukia kisa hicho”
“Kumbe je?”
“Tuendelee kuwa marafiki hivihivi”
“La…”
Kabla ya Sebastian kumalizia anachokiongea walitokea watu wawili na kukaa pembeni yao,mmoja aliketi pembeni ya Nasra na mwingine pia hivyohivyo kandokando ya Sebastian.
“Mbona,mnakuwa sio wastarabu.Tuna mazungumzo yetu”
Sebastian akaropoka lakini akashtuka na kuogopa baada ya kuona bastola imetolewa chini bila mtu yoyote kuona.
“Sikilizeni,taratibu inukeni.Sitorudia tena”
Ilikuwa ni kauli kutoka kwa mwanaume aliyekuwa kandokando ya Sebastian,alikuwa ni mzungu aliyenyoa nywele zote yaani upala.
“Inukeni wote,haraka”
Sebastian hakuelewa watu hao walitaka nini.
“Nina dolla laki moja nitawapa”
Kutokana na utajiri wa baba yake alidhani wenda wanataka pesa.
“Hatuna shida na pesa zako,simama upesi”
Nasra hakuachwa nayeye akainuliwa, bastola zilikuwa nyuma ya migongo yao bila mtu yoyote yule kuona,wakatolewa nje na kuingia ndani ya gari walilokuja nalo watu hao waliowaweka mateka.
Nasra alitetemeka kupita kiasi,aliogopa kufa.

* ****
Sebastian na Nasra walifikishwa ndani ya nyumba kubwa ambayo haikumaliziwa bado,wakapigishwa magoti na mikono yao ilikuwa hewani.
“Sebastian”
Sauti nyingine ilimshtua kutokea nyuma yake,mwanaume aliyemuona alimfahamu vizuri tu.
“Habib,mzigo wako nitakuletea upaswi kufanya hivi.Embu tuongee kiume”
“Siwezi kuongea tena,nilikupigia kelele sana ukaniona fala sio?Sasa leo ninakuuwa”
Kwa picha ya harakaharaka watu waliowazunguka Sebastian na Nasra walikuwa watumiaji wakubwa wa madawa haramu ya kulevya aina ya Coccaine na Herroin.Jitu hilo lilimuangalia Nasra na kumsogelea karibu.
“Vua nguo zako binti”
Habib alisema,sauti hiyo ilisikika lakini Nasra akabaki amenyamaza kimnya.
“Nimekwambia vua nguo zako”
“Jamani,huyu mwanamke hausiki…..”
Sebastian alijaribu kutetea lakini alitulizwa na kitako cha bastola akadondoka chini chali,mdomo wake ukawa umepasuliwa vibaya sana,damu zikamtoka kama mchuzi.
“Kacha kacha”
Bastola ilikokiwa,Nasra akanyooshewa usawa wa kichwa.
“Paaaaaaaaaaa”
Mlio wa bastola ulisikika,Sebastian aliyekuwa chini alishtuka na kugeuza shingo yake Nasra alikuwa chini.Isingekuwa Habib kupindisha mkono wake pembeni wenda risasi hiyo ingefumua ubongo wa Nasra mara moja,risasi ilimkosa kosa na kumpitia karibu na sikio lake la kulia.
“Simama vua nguo zako,mara hii nakuuwa”
Ilikuwa ni kauli nyingine,Nasra aliyekuwa chini alihisi ngoma za masikio yake zimepasuka.Alihisi kinyesi kinataka kumtoka,alijuta kutoroka na kufika Marekani.Haraka akaanza kutoa nguo ya juu,akavua sidiria yake.Akatoa suruali aliyokuwa amevaa,akabaki na chupi.
“Hiyo chupi unamuachia baba yako aje akuvue au?”
Nasra huku akilia machozi,alitoa nguo yake ya ndani.Akabaki kama alivyozaliwa.

***
Mziki ulikuwa unakita ndani ya club Maisha,ukumbi ulikuwa umejaa sio masihala.Kila mtu alitaka siku hiyo kwenda kutoa mawazo baada ya siku saba za kazi kuisha.Hapo ndipo Alex na Sonia walifika ili kujirusha,Alex alishaamua kuweka mapenzi yake kwa mwanamke huyo na alitaka kumuoa kabisa.
Ndiyo maana hakuwa na habari tena na Latifah,aliamini ipo siku atamsahau,uzuri wa Sonia ulikuwa wa kutisha na ulitingisha kila alipopita,kila mtu alimshangaa yeye,Alex akavimba kichwa akawa anatanua mikono yake.Akajiona yeye ndiye yeye,hakuna mwingine zaidi yake.
“Broo Alex”
Ni sauti iliyomshtua kutoka kaunta,alivyogeuka akacheka na kukumbatiana na mwanaume aliyemuita kwa furaha.
“Stuwart ndugu yangu?Umerudi lini?”
“Wiki iliyopita”
“Enhee,za Iringa?”
“Huko safi,baridi tu vipi shemeji hajambo?”
“Yeye mzima”
Alex alificha hakutaka mambo yake yajulikane kwa ndugu zake wengine,japokuwa Stuwart alikuwa ndugu yake wa damu,mtoto wa Baba yake mdogo.
“Anhaa,alafu msalimie rafiki yangu huyu, anaitwa Hafuan”
Alex alianza utambulisho,Stuwart akamtizama Sonia akionekana kama anamfananisha.Akamuangalia kwa umakini kuanzia juu mpaka chini.
“Mbona kama anafanana na binti fulani hivi anaitwa Sasha”
Stuwart akauliza lakini Sonia akajifanya hajasikia chochote.
“Wawili wawili hapa duniani bwana”
“Sio kufanana huku aisee”
“Any way,wakupe kinywaji gani?”
Alex hakutaka mazungumzo hayo yaendelee ndio maana akabadili mada.

Stuwart alinunuliwa bia akatulia na mziki uliendelea kupigwa,jicho lake moja lilikuwa kwa Sonia anamkagua, alimuangalia kwa kuibia ibia huku akiwa na bia yake iliyokuwa kwenye glasi,uzuri wa msichana huyo ulimpagawisha ndiyo maana alizuga kama anamfahamu ili kuangalia upepo unaenda vipi.Kitendo cha simu ya Alex kuita na kutoka nje kwake ilikuwa kama ‘ahsante Mungu’ akamsogelea Sonia karibu na kumgusa begani.
“Chaurembo,mambo vipi?”
Stuwart alianza maongezi kwa Mbwembwe.
“Poa”
“Huyu ni kaka yangu,ndio bwana ako nini?Ana mke huyu ujue.Ana watoto wawili”
Stuwart alianza kujipigia debe kwa njia ya kumkandia ndugu yake,hakuelewa jambo analofanya lilikuwa ni sawa na kujichimbia kaburi mwenyewe.
“Kumbe ana mke?Mimi mbona kanidanganya kwamba hajaoa”
Sonia nayeye akaweka usanii,akajifanya hajui lolote.
“Muongo,kama anakutaka usimkubali kabisaaa.Achanaaa nayee kaa naye mbalii.Hafaii kabisaaaa.Alafu sasa nipe namba zako”
“Huyu nani yako kwani?”
“Ndugu yangu wa damu,mpwa wangu huyu”
Stuwart alijiingiza mwenyewe ndani ya kumi nane za Sonia,ukimwi ulikuwa unamuhusu bila kujiuliza chochote akachukuwa simu ya Stuwart na kuziandika namba zake kisha kumrudishia simu.
“Sasaaa,hii ndiyo club nayokwambia huwa napatikana hapa huyu ni ndugu yangu kabisaaa,baba mdogo na baba mkubwa”
Stuwart alibadilisha mazungumzo baada ya Alex kutokea,alijihisi yeye ni Christian Ronaldo tena kapiga bao la kisigino kumbe alikuwa akijitumbukiza mwenyewe kwenye shimo kubwa.
“Koho koho kohoo”
Sonia alipaliwa na kinywaji chake,kuna mtu alimuona mbele yake aliyemshtua.Alikuwa ni Shadrack mwanaume aliyembaka na kutaka kumuuwa hotelini.Ndiyo maana akashtuka.
“Hafuan vipi?”
Alex akauliza.
“Naomba tuondoke”
“Tatizo nini?”
Shadrack akafika mpaka kaunta alimuona mwanamke anayekohoa kainamisha kichwa chake chini.
“Vipi kaka?Mpeleke nyumbani.Anaumwa au?”
Shadrack alitia neno baada ya kumuona mwanamke huyo anakohoa,kapaliwa na pombe.

 Kichwa alikielekezea chini kwa maana hiyo alikuwa anatizama viatu aina ya mkuki moyoni alivyovaa Shadrack mbele yake,kitendo cha kuinua uso wake kingemaanisha kuonekana.Hakutaka kitu hicho kitokee, alimuogopa Shadrack sababu aliogopa kifo ndiyo maana akabaki anaangalia chini akijifanya anakohoa.
“Una tatizo gani Hafuan?”
Mr.Alex ndiye aliuliza akimpiga piga Sonia mgongoni,lakini badala yake Sonia akiwa hivyohivyo tena kwa kujikoholesha akaanza kuwapangua watu akitafuta upenyo wa kutoka nje, kwa kitu alichokifanya aliamini ndiyo njia pekee ya kutoka eneo hilo hatari,alitoka mpaka nje ambapo alijifanya kukohoa tu.
Mr.Alex alikuwa nyuma yake.
“Vipi Darling?”
“Kifua kimenibana,naomba turudi nyumbani sasa hivi”
Aliongea hivyo akiwa tayari anaangaza huku na kule anatafuta sehemu walipopaki gari yao.
“Twende basi tukamalizie kidogo”
“Alex kama hutaki niambie nirudi mwenyewe”
“Okay sawa,ngoja nikamuage ndugu yangu”
“Nakusubiri”
Alex aliingia ndani ya club na baadaye alivyotoka walizama ndani ya gari na safari ya kurudi Afrikasana ikaanza.
***
Siku mbili nzima Sonia alikuwa akilala nyumbani kwa Alex,kupika na kupakua.Walikuwa ni kama mume na mke japokuwa ndoa haikuhalalishwa.Sonia alifanya kila kitu kama mke,alipika,alimfulia Alex na kufanya naye ngono asubuhi,mchana na usiku.Hiyo ilitosha kabisa kumshawishi Alex kuwa Sonia ndiye mke mwingine wa kuoa,alimpenda mazima na alijuta kuoa mapema.Kitu kilichokuwa kinamuuza kichwa Sonia ni ujauzito aliokuwa amebeba tumboni,jambo hilo alipolikumbuka ndiyo lilimvuruga akili na kumuharibia mudi kabisa.
“Baby vipi?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Alex siku hiyo usiku wakiwa kitandani,Sonia alikuwa ni mwenye mawazo.Macho yake yalikuwa yanatizama darini!
“Darling…Hafuan Una tatizo gani?”
Alex akauliza tena lakini Sonia hakumsikia mwili wake ulikuwa kitandani lakini akili yake ilikuwa mbali sana.
“Hafuan”
“Abeee..Abeee”
“Vipi?”
“Safi,hamna kitu”
“Una tatizo gani?”
“Sina tatizo.Kuna kitu nawaza hapa”
“Kitu gani?nishirikishe basi”
“Usijali Love”
“Niambie mpenzi wangu”
“Nakuwaza wewe”
“Unaniwaza kwanini?”
“Wewe ni mme wa mtu,ipo siku utanifukuza na kumrudia mkeo”
“Siwezi kufanya hivyo.Tena ngoja nikwambie kitu nilishukuru sana ulivyompigia simu kumtukana.Nakupenda Hafuan najuta kwanini hata nilioa mapema”
“Kwanini unanipenda ivyo?”
“Sijui lakini nina imani ni Mungu”
Kupitia macho ya Alex Sonia alijifunza kitu kuwa Alex alikuwa ana mapenzi ya ukweli tena alikuwa amekolea sio masihala,alimsikitikia sana mwanaume huyu ambaye hajui lolote,alielewa kwamba asilimia mia moja alishampa ukimwi kwa maana hiyo alikuwa ni mfu tayari anayetembea.
“Nakupenda Alex”
Sonia akajilegeza utadhani alimpenda Alex kumbe haikuwa hivyo,siku zote moyo ni giza kinene.Maneno ya Sonia yalipita ndani ya masikio ya Alex na kumsisimua mwili wake,alivyomtizama Sonia akahisi jogoo wake taratibu anapanda mtungi,hapohapo akamsogelea mdomoni wakaanza kulana denda.
Damu ya Alex ilimuenda kasi na alifikiria ngono kichwani mwake,Sonia alilijuwa hilo akazidi kuuzungusha ulimi wake ndani ya mdomo wake huku akimpapasa mwilini mwake hususani masikioni,mambo hayakuishia hapo kilichoendelea hapo ni kuvuana nguo na kuzitupa kando.Alichofanya Sonia ni Kumuweka Alex chini yeye akapanda juu yake,akashika ndizi vizuri na kuichomeka ndani ya mgodi wake.Alex aliyekuwa chini alikishika kiuno cha Sonia na kuhisi raha za ajabu,hazikupita hata dakika tatu Alex akawa tayari amemwaga oil chafu,ametulia jasho kwa mbali linamtoka.
“Baby,sorry nimewahi kufika”
“Sawa usijali,ilimradi umefurahi kuhusu mimi usijali”
Waliingia kuoga na baadaye kurudi kitandani kulala.
****
Sonia alipigwa na butwaa alivyoamka asubuhi akiwa na nguo ya kulalia alivyofika seblen,alikuta wazee wawili na wakina mama watatu wamefunga ushungi kichwani alivyoangalia kushoto kwake alimuona Mwanamke maji ya kunde analia machozi mkononi kabeba mtoto mchanga,ugeni huo aliuelewa sana kupitia mwanamke anayelia ingawa hakuwahi kuonana naye kabla.
Kila mtu alimtizama kwa macho makali.
“Mambo zenu”
Sonia akatupa salamu kwa nyodo,tena bila kuogopa lolote lakini badala yake alijibiwa na msonyo mkali tena wa mwendokasi!
“Tuitie Alex”
Mzee mmoja wapo alitoa kauli hiyo,Sonia akamtizama bila kujibu chochote akatembea kwenye korido na kufungua mlango.
“Baby kuna wageni wako”
“Wakina nani?”
“Mimi siwajui”
Sonia alijifanya hajui lakini alijua fika kwamba aliyekuwepo Seblen ni Latifah pamoja na ndugu zake wamefika.
“Hujawauliza?”
“Hapana”
“Okay nakuja”
Alichofanya Alex ni kuvaa shati na kuvuta kaptula yake,akaweka mwilini vizuri na kufungua mlango kuelekea Seblen,butwaa alilopigwa halikuwa na mfano wake ingawa hakutaka kujionyesha waziwazi.
“Shikamooni”
“Kuwa nawewe upate yako”
Hilo ndilo jibu alilopewa na mwanamama aliyekaa kushoto kwa Latifah.
“Hivi wewe Alex,unajionaje labda?”
Lilikuwa ni swali lililotupwa kwa shari.
“Mama Amina,embu punguza jazba.Hatujaja kubomoa hapa tumekuja kujenga”
Mzee mwenye busara akaingilia kati.Muda wote Latifah alikuwa akilia machozi ya kwikwi alimpenda sana mume wake kila alipomuangalia alihisi kuumia moyo.
“Mwanangu Latifah amefanya kosa gani?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa mzee mwingine aliyekuwa amevaa kanzu nyeupe na kibalakashee kichwani,Alex alimtambua vizuri alikuwa ni baba mzazi wa Latifah, Mzee Daudi Mwijuma.
“Hajafanya kosa mzee wangu”
Alex akajibu kwa busara zote,roho ya huruma ilimuingia, alivyomuangalia mwanaye anayelia ndiyo kabisa akajihisi ni mkosaji machozi yakamlenga akamtizama mke wake jinsi alivyokuwa ana sura ya upole.
“Naelewa ni mambo ya kidunia sawa, hatutaki kujua ni nani mwenye kosa lakini nachokuomba ulifikirie hilo swala mara mbilimbili hata quran takatifu imekataza maswala hayo,embu tizama mtoto wako mchanga anavyolia,huyo ni malaika wa Mungu analia hapo kwa ajili yako”
Maneno ya Mzee Daudi yalimchoma Alex mtima, akajikuta ameganda kama barafu hakuelewa ni kitu gani akifanye alibaki akimtizama mke wake Latifah,alijihisi ni mkosaji mbele za Mungu wake aliye juu Mbinguni.
“Lati..fah”
Hatimaye akamuita na kumsogelea.

Kila kilichozungumzwa Seblen Sonia alikisikia sababu alikuwa amesimama kandokando ya kordo amejibanza,kusamehewa kwa Latifah na kurudi nyumbani hapo kulimaanisha kupewa virusi vya Ukimwi, bado hakutaka swala hilo litokee ndiyo maana akatokeza mpaka kwa Alex,bila aibu yoyote akaenda kumkalia juu ya mapaja.
“Baby,upo bize sana?”
Sonia aliongea kimahaba na kumfanya Alex apatwe na Kigugumizi,Sonia alimgeukia Mzee Daudi akampandisha juu mpaka chini kwa dharau,hakutofautishwa na mtu anayetizama kinyesi, hapohapo akaachia msonyo.
“Mizee mingine bwana”
Sonia alijisemea kwa sauti.
“Hafuan,ingia ndani tafadhali”
Alex akaongea taratibu kwa sauti ya chini.
“Alex no,leoleo naomba uniambie sasa hivi unanipenda mimi au huyu kibwengo wako?”
Sonia akapayuka kwa sauti.
“Hafuan lak..”
“Niambie chagua moja unanipenda au?”
Lilikuwa ni swali lililokuwa wazi lakini jibu lake halikuwa rahisi kutoka kwa wakati huo,Alex alikuwa katika wakati mgumu sana.Wazee wakatizamana.Wakina mama wakamkata Sonia jicho kali.
“Wewe kahaba”
Mwanamama mmoja akashindwa kuvumilia akarusha tusi.
“Kahaba mwenyewe”
“Unasemaje wewe kibiritingoma?”
“Kama ulivyonisikia”
Sonia alianza kutoa maneno machafu kwa akina Mama akawa mkali kama pilipili,laiti kama wangelijua nia ya Sonia kufanya hivyo wangemshukuru sana lakini badala yake walizidi kumtukana matusi.
“Wewe mwanamke mse** nini”
“Eh eh eh eh sasa sikilizeni embu tokeni kwangu,fanyeni upesi”
Alex aliingilia katikati na kusimama wima,matusi aliyokuwa anatupiwa Sonia yalizidi kipimo hakutaka kuendelea kusikia anatukanwa mbele yake.
“Nasema hivi.Tokeni nyumbani kwangu”
“Lakini shemeji nakwambia kitu kimoja utatukumbuka,ipo siku utatukumbuka tu”
“Embu nendeni,tokeni nje.Aya Mzee viatu vyako hivi hapa”
Kitendo hicho kiliwafanya wazee hawa waache laana kubwa sana na waliondoka huku wakiteta.
“Baby umeoona nimetukanwaaa!”
Sonia alianza kudeka baada ya wageni kutoka nje,alimfuata Alex na kumkumbatia.Moyoni alijiona mshindi kupita kiasi,hakuamini kama ni yeye ndiye kafanya usanii huo.Licha ya yote hakuwa na kosa aliamini jambo alilolifanya lilikuwa sahihi kabisa.
***
Ni kweli alimpenda Sonia ndiyo maana alidiriki hata kuwafukuza wakwe zake,hakuelewa alikuwa anafanya jambo la kipumbavu,uzuri wa Sonia ulimchanganya akawa kama amerogwa ama amewekewa limbwata,kila alichosema Sonia alitekeleza mara moja,akawa ameshikwa pembe.
“Baby nina safari kikazi”
Siku hiyo Alex alirudi mapema na kumueleza Sonia.
“Unaenda wapi?”
“Uganda”
“Sasa inakuwaje?”
“Tunaenda wote”
“Real?”
“Yeah,kwahiyo anza kujiandaa”
“Sawa love,safari ni lini?”
“Wiki ijayo Jumatano”
“Okay love inabidi nijiandae,leo nitaenda kwangu basi au?”
“Okay sawa.Una pesa?”
“Hapana”
Alex akaingia ndani ya kabati na kutoa bahasha,akaanza kuzihesabu pesa na kuchomoa kibunda cha noti za elfu kumi kumi yaani laki moja, akamkabidhi Sonia.
“Utachukuwa taxi”
“Okay baby”
Sonia alijiandaa siku hiyo mchana na baada ya hapo alielekea nyumbani kwake Mikocheni B.

Alivyofika alijitupa kitandani akiwa amechoka,akachukuwa simu yake na kuiwasha.Ilivyowaka tu meseji ziliingia nyingi mfululizo.nyingi zilitoka kwa wanaume wakimtongoza na wengine wakitaka kumpa ofa,katika meseji zote alizosoma moja kati ya hizo zilimfanya agandishe macho yake.
‘MREMBO UKIPATA UJUMBE WANGU NAOMBA NITAFUTE NILIJARIBU KUKUPIGIA LAKINI HAUKUWA HEWANI,MIMI NI STUWART TULIKUTANA CLUB NDUGU YAKE NA ALEX’
Aliitizama meseji hiyo kwa umakini na kutabasamu.
“Hawa wamekwisha”
Sonia alijisemea na kuipiga namba ya Stuwart akasikia inaita.
“Halloo,mambo vipi?”
Upande wa pili wa simu ulisikika.
“Poa”
“Ulipata ujumbe wangu?”
Stuwart alianzia mbali kidogo.
“Ndiyo nimewasha simu sasa hivi”
“Kwanini sasa ulizima?”
“Simu yangu mbovu,niliipeleka kwa fundi juzi lakini naona bado haijapona”
“Uko wapi?”
“Nipo hostel”
Sonia alidanganya!
“Anhaa,sasa unapajua posta?”
“Posta sehemu gani?”
“Posta mpya hapa,samora avenue katikati kuna askari kashika mtutu”
“Hapo napajua”
“Njoo maeneo haya,nataka nikununulie simu mpya”
Picha ya Sonia ilimpitia kichwani uzuri wa msichana huyo haukuwa wa kawaida machoni mwake ndiyo maana alivyosikia simu yake mbovu alitaka kumuhonga ili amvute karibu, hakuelewa kuwa anaenda kuukumbatia mzinga wa nyuki.
“Sawa ahsante kwahiyo nije sasa hivi?”
“Sawa wewe njoo”
“Sina nauli,Mama hajanitumia pesa”
Sonia alijuwa kuchuna na kwa jinsi Stuwart alivyoingia na gia yake ilikuwa ni lazima amchune kwanza.
“Una tigo pesa?”
“Ndio”
“Nakutumia nauli sasa hivi uje”
“Sawa”
Stuwart alishuka gorofani harakaharaka mpaka kwa wakala aliyekuwa karibu akatoa noti tano za elfu kumi mfukoni.
“Oya Biko nataka kutuma pesa”
“Tigo au Voda?”
“Tigo”
“Bei gani?”
“Elfu hamsini”
“Hiyo sina,labda nenda pale mbele kwa Dani”
“Poa”
Stuwart hakuchoka alitembea mpaka mbele ya kibanda kinachofuata akamtumia Pesa Sonia,ili kuhakikisha alimpigia simu.
“Sawa basi uje”
Stuwart alijichekesha akajua tayari kamnasa mwanafunzi wa chuo.
***
Ni kweli Sonia alinunuliwa Simu kubwa aina ya Samsang Galaxy s6, Kwa Stuwart alidhani hiyo ndiyo ilikuwa mwisho na tayari ndoano yake ilifanikiwa kuvua samaki.
“Simu ni nzuri ahsante sana”
“Usijali hivyo ni vitu vidogo sana kwangu”
“Ahsante sana,hivi unaitwa nani tena?”
“Stuwart,sema hapa kazini wamezoea kuniita tajiri mtoto”
“Kwanini wanakuita hivyo?”
“Tuachane na hayo,leo upo bize sana?”
“Ndio lakini sio sana”
“Leo inabidi uje kwangu upajue”
“Unaishi wapi kwani?”
“Kijitonyama”
“Sawa,lakini nitawahi kurudi”
“Hakuna tabu”
Siku hiyo Stuwart alifanya kazi zake harakaharaka akiwa amemuacha Sonia kwenye moja ya mgahawa baada ya hapo alimfuata,wote wakaingia kwenye gari na safari ya kwenda Kijitonyama kuanza.
“Alex ulionana naye?”
Stuwart alivunja ukimnya.
“Hapana tangu siku ile alivyonirudisha Hostel sikumuona tena”
“Hivi mlijuana wapi?”
“Nilishawahi kufanya field ofisini kwake”
“Ana mke yule unajua”
“Najua alafu ananitaka,kwani kaka wewe hujaoa?”
“Mimi bado”
Maongezi yaliendelea ndani ya gari mpaka walipofika Kijitonyama nje ya nyumba iliyozungushiwa ukuta mfupi,wote wakashuka na kuingia mpaka ndani.
“Hapa ndio kwangu,alafu sijakujua jina lako ujue”
“Kweli?”
“Ndio”
“Mimi naitwa Rashidah”
“Rashidah?Rashidah Wanjara au?”
Stuwart akatania wote wakacheka,Stuwart aliendelea kumtizama Sonia kwa macho ya matamanio.
Akamsogelea karibu na kumgusa kiuno,kilichomfurahisha aliona Sonia katulia hajigusi, hapo ndipo alipo mvuta karibu yake kabisa akaanza kumla denda alikuwa ni kama amejiandaa vile,maana aliupokea ulimi wa Stuwart vizuri wakaanza kubadilishana mate,hapohapo juu ya kochi walianza kuvuana nguo na kushikana shikana.
Sonia tayari alikuwa amemnasa Stuwart,akafanya naye mapenzi pekupeku yaani bila kondom kwa maana kuwa ukimwi ulikuwa nje nje.
****
“Hodi humu ndani”
“Karibu shemeji,pita ndani”
“Vipi ulikuwa umelala nini?”
“Nilikuwa nimepumzika na wifi yako sijui mke mwenza wako.Vipi mtoto yupo wapi?”
“Nimemuacha kwa Amney”
“Kwa Amney?kwani hujatokea nyumbani?”
“Mh,kwani shemeji wewe hujui nimeachana na kaka yako?”
“Hapana sio kweli”
“Sina sababu ya kukudanganya,kapata mwanamke mwingine.Hajakutambulisha?”
“Ah wapi,mara ya mwisho nilikutana naye club kama wiki mbili zilizopita”
“Basi ndiyo hivyo shemeji”
Latifah alifika nyumbani kwa Stuwart na alizoea kumuita shemeji sababu Alex alikuwa na undugu naye.
“Mimi nitaongea naye”
“Haina ha…”
Kabla ya Latifah kumalizia sentensi yake aliona kitu kilichomshtua,Sonia alikuwa akitokea chumbani kwa Stuwart, moyo wake ukapiga paa!hakuelewa kuwa macho yake yanamdanganya au anaota ndoto ya asubuhi!


 Latifah alizidi kumuangalia Sonia mara mbili mbili,upande mwingine wa akili yake ulimwambia kuwa alimfananisha lakini moyo wake ulikataa katakata, haikuwezekana hata kidogo kwa binadamu wafanane kwa kila kitu,mwanamke aliyemkuta kwa mume wake Alex siku chache na kuwatukana dada zake ndiyo huyo alimuona pia nyumbani kwa Shemeji yake, Stuwart.
Sonia aliyekuwa Seblen sio kwamba hakumuona Latifah,aliendelea kuzuga na kuonekana akitafuta kitu ambacho hakikujulikana.
“Shemeji,huyu mwanamke umemtoa wapi?”
Latifah alimuuliza Stuwart kwa sauti ya chini kidogo lakini Sonia alisikia.
“Vipi kwani?Unamfahamu?”
Stuwart badala ya kujibu akauliza swali,likawa swali juu ya swali.
“Mimi namfahamu ndio”
“Ulishawahi kumuona wapi?”
“Nyumbani kwa mume wangu,huyu ndiye alifanya mpaka nimeachika”
“Shemeji”
“Stuwart naomba unisikilize,huyu mwanamke ni shetani”
Maneno ya Latifah yalimuingia vizuri sana Stuwart aliyekuwa amekaa kitako anamsikiliza,alijaribu kuunganisha matukio mbalimbali,akamgeukia Sonia aliyekuwa bado bize anatafuta kitu ambacho hata hakikujulikana.
“Umesema ilikuwaje?”
“Alimtukana baba yangu vibaya sana kama unabisha mpigie simu Alex sasa hivi au mimi nimpigie?”
“Subiri kwanza mimi nitajua cha kufanya”
Habari alizopewa siku hiyo zilimchanganya kichwa chake,alikuwa ameshea tayari na ndugu yake.Hakuumia sana moyo kwa kitendo hicho, kilichomvuruga ubongo ni kuingizwa mjini kwa kuongopewa.
“Sawa nitalishughulikia hilo shemeji yangu”
Stuwart hakutaka kuendelea na mazungumzo na wala hakutaka kumuita Sonia kwa wakati huo,alisubiri mpaka Latifah aondoke ili amtupie maswali Sonia,alitaka kujua kuwa ni kweli ana mahusiano ya kimapenzi na ndugu yake, Alex.
“Aya shemeji mimi naenda ngoja nimuwahi mtoto”
“Sawa shemeji”
Mlango ulivyofungwa tu.Akasimama wima na kumuendea Sonia aliyekuwa kwenye friji anajifanya kupanga vitu.
“Rashidah”
“Abee love”
Sonia aligeuka na tabasamu akijifanya kama hajui lolote.
“Kumbe unatembea na Alex?sasa kwanini uliamua kunidanganya?unamjua yule mwanamke?”
Yalikuwa ni maswali aliyotupiwa Sonia mfululizo hakuelewa aanze kujibu lipi.
“Baby”
“Niambie ukweli kwanza”
“Stuwart mimi nakupenda sana,nilifanya hivi ili nisikukose.Alex niliwahi kutembea naye ndiyo lakini haikuwa kwa ridhaa yangu.Yule ni mke wa Alex ndiyo namfahamu.Nakupenda Stuwart naomba tuachane na hayo”
Sonia aliongea kama kasuku na katika maneno aliyokuwa anaongea hakuna hata moja wapo lililokuwa na ukweli ndani yake,alifanya hayo yote sababu hakutaka agundulike mapema.
Zaidi na hayo alikamua machozi mililita moja ili kusindikizia uwongo wake,akamsogelea Stuwart midomoni na kumnyonya lips.
“Stuwart nakupenda sitaki uniache,samahani kwa kukudanganya naomba uwe mwanaume wangu wa mwisho nataka unioe.Wanaume wamenitesa sana ndiyo maana wamenifanya nikawa muongo kiasi hiki,umenisamehe?”
Sonia alikuwa kama yupo kwenye bongo movie kila alichokuwa anakifanya kilikuwa ni maigizo tu,akafanikiwa kuununua moyo wa Stuwart.
“Usijali Rashidah,futa machozi”
Stuwart alijibu huku akimshika Sonia mashavuni,hakuelewa lolote juu ya mwanamke huyo hatari anayesambaza ugonjwa wa ukimwi.
“Umenisamehe?”
“Ndio mpenzi wangu”
“Nakupenda Stuwart”
Hapohapo wakaanza kunyonyana midomo yao taratibu sana,Sonia alijiona bab kubwa!Nyonga za Sonia zikakamatwa akainuliwa na kuwekwa juu ya meza ya chakula huku wakiendelea kushushiana mabusu,shingo yake ikakamatwa ikaanza kulambwa.Ilikuwa ni asubuhi ya saa moja Sonia alikuwa amevaa kanga tupu,Stuwart akaitoa akaanza kuyanyonya maziwa ya mwanamke huyu.
Hapo ndipo ulikuwa udhaifu wa Sonia akabaki ametulia na damu ikaanza kumuenda mbio kuliko kawaida,akahisi kama shoti ya umeme inapita mwilini mwake kazi yake ikawa ni kumshika Stuwart kichwa chake akihisi raha za ajabu kupita kiasi!Mambo hayakuishia hapo,Stuwart alishusha mkono wake mmoja mpaka kwenye kitovu akazidi kuuporomosha ukafika mpaka mabondeni,akaanza kucheza na mgodi wa Sonia.
“Griii griiiiiii”
Simu ya Stuwart ndiyo iliyomshtua ikiwa mfukoni mwake,alivyotaka kuitoa Sonia alimzuia hakutaka akatishwe raha yake ambayo tayari alikuwa ameanza kuipata.Simu iliendea kuita tena,ikakata na kuita tena wala haikupokelewa,hazikupita sekunde mbili simu ya Sonia pia ikaanza kuita.
Hapo ndipo walianza kuhisi kuwa mtu anayepiga alikuwa ni Alex hata hivyo walipuuzia.

Wakaendelea na kibarua chao,raha walizokuwa wanapata hazikuweza kuelezeka kiwepesi.Waliendelea kupigana madenda wakilambana kila sehemu.Isingewezakana hata kidogo kwa Stuwart kuamini kwamba anammiliki mwanamke mrembo kama Sonia ambaye hata lingetokea shindano la Miss Tanzania mwanamke huyo angetwaa taji la urembo,Sonia alikuwa ni mzuri kupita kiasi,mwili wake ulivutia hasa alipotoa nguo zake zote sababu alikuwa mweupe mno na hakuwa na doa lolote lile.Ndiyo maana hata Stuwart alikuwa yupo radhi kugombana hata na kaka yake ili awe na Sonia.

****
“Unataka nini?”
Ilikuwa ni simu iliyopokelewa na Akex akiwa ofisini kwake asubuhi,amevaa shati jeupe yupo nyuma ya meza kubwa.
“Alex naomba nisikilize mume wangu”
“Mimi nawewe si yamekwisha tayari,mbona unakuwa sio mwelewa?”
Latifah alizungumza kwa sauti ya upole kama kawaida yake upande wa pili wa simu.
“Sawa umeniacha lakini haina haja ya kuwekeana mabifu,utabaki kuwa mume wangu tu.Naomba nikwambie kitu kimoja”
“Kitu gani?kama kuhusu watoto nitakuwa natuma pesa”
“Kuhusu huyo mwanamke wako,sasa hivi yupo na Stuwart.Yaani ninavyoongea nawewe nimewaacha Kijitonyama,sikudanganyi na unajua tangu uwe mume wangu sikuwahi kukudanganya”
“Mwanamke gani?”
“Mwanamke wako”
“Hapana utakuwa umemfananisha”
“Siwezi”
“Sawa ahsante”
Alex akashusha pumzi ndefu ya ndani kwa ndani,maneno aliyoambiwa na Latifah hakuyaamini lakini alitaka kuhakikisha,akachukuwa simu nyingine pembeni yake na kuitafuta namba ya Stuwart.
Kitu kilichomchanganya akili yake simu iliita bila kupokelewa,ikaita tena lakini mambo yakawa hivyo hivyo.Kijasho kikaanza kumtoka hakutaka kuamini moja kwa moja kuwa Sonia atakuwa na Stuwart,ndiyo maana alivyokata simu alimtafuta na Sonia pia hewani lakini mambo yalikuwa yaleyale simu ya Sonia haikupokelewa,hilo ndilo likamchanganya akili zaidi.
Alimpenda sana Sonia na ndiyo maana akachukuwa maamuzi magumu ya kumtukana Baba mkwe wake na kumfukuza mkewe wa ndoa.
“Bosi kuna mafaili hapa unatakiwa kusain…..”
“Baadaye”
Sekretari aliingia ofisini kwa Alex akiwa na jambo la muhimu.
“Lakini bosi una..”
“Beti nadhani nimeeleweka,kesho tafadhali sasa hivi ninatoka.Mwambie Nicholus kikao leo hakuna aandae kesho”
Alex aliongea na kuvuta koti lake la suti lililokuwa nyuma ya kiti chake akampita sekretari wake.Alivyofika mlangoni akageuka na kurudi, alionekana kuna kitu amesahau,alifika kwenye meza yake akavuta ‘draw’ na kutoa bastola yake.
Sio kwamba alitaka kwenda kuitumia lakini kwake hiyo ilikuwa ni kama ‘self defense’ kila wakati alikuwa nayo.Akaiweka kiunoni vizuri tena mbele ya Beti na kuifunika na koti kisha kutoka nje,akashusha ngazi mbilimbili mpaka kwenye parking ya magari huku akijaribu kuipiga simu ya Sonia,lakini bado haikupokelewa.
Kwa kuwa aliambiwa kuwa alionekana kijitonyama hivyo aligeuza gari ili aelekee nyumbabni kwa Stuwart,hakuelewa ni kitu gani angekifanya endapo atakuta kitu ambacho hakukitarajia,alijuwa jinsi gani alivyokuwa na hasira chafu ndiyo maana alimuomba Mungu sababu hakushindwa kutumia bastola kufanya kitu chochote kibaya.
Kwake siku hiyo ilikuwa ni kama bahati hakukuwa na foleni yoyote ile,alitokea njia ya sinza na kukunja kona alivyofika sheli ya Total,nyumbani kwa Stuwart alipafahamu sana.
Akaingia barabara ya vumbi bila kupungunza mwendokasi,akaweka gari kando baada ya kufika kandokando ya ukuta mfupi,bila kujifikiria akashuka.
Gari ya Stuwart aina ya Verosa ilikuwa nje kumaanisha kuwa alikuwepo ndani na hapo ndipo alipofungua geti lililokuwa limeegeshwa,mapigo yake ya moyo yakazidi kumpiga kwa nguvu baada ya kukuta viatu ambavyo alivijua kabisa,vilikuwa vya Sonia hapo ndipo jasho la hasira lilizidi kumpanda.Akazungusha kitasa lakini mlango ulikuwa umefungwa kwa ndani.
“Stuwart,Wewe Stuwart”
Alex aliita huku akitembea mpaka dirishani akachungulia.

****
“Ahhh aaah sshhhs aaaaah aaassshh Stu….wa..rt aaaaah I lo…ve y..ou aah aaah aaah”
Sonia ndiye alikuwa akitolea sauti puani akiwa juu ya meza,wanafanya ngono.Kwenda chumbani kufanya tendo hilo waliamini ulikuwa upotevu wa muda.Ndio maana miguu ya Sonia ilikuwa imejifiringisha kiunoni mwa Stuwart wana njunju!
Kila kilichotokea siku hiyo kwa Stuwart alizidi kuamini kuwa yupo ndotoni,ndiyo maana hata alivyofika mshindo hakuamini aliendelea kumpiga madenda Sonia aliyekuwa yupo hoi jasho linamtoka kwa mbali.
“I love you Stuwart”
Sonia alisema kwa sauti ya chini tena ya huba.Jinsi macho yake alivyoyalegeza ndiyo ikamfanya Stuwart apagawe zaidi.
“Griiii griiiii”
Simu ya Stuwart iliita tena, safari hiyo ndipo alipobutuka akainama chini na kuiokota suruali yake,akaitoa simu iliyokuwa mfukoni.
“Yesu wangu bosi huyu,Mungu wangu”
Suwart alikema na kuhaha alivyotupa macho yake juu ya saa ya ukutani aligundua kuwa amechelewa masaa mawili kazini na alihitajika kusaini hundi za ofisini asubuhi ya saa moja.
“Hallo bosi za asubuhi?”
“Upo wapi?”
Bosi wake aliuliza swali,bila kupokea salamu
“Mimi,ni ni ni nipo kwenye foleni hapa daraja la salenda”
“Paki gari pembeni chukuwa pikipiki upesi uwahi ofisini,ukasaini zile cheki zinahitajika sasa hivi”
“Sawa bosi”
Bila kupiga porojo wenda siku hiyo ndiyo kibarua chake kingeota nyasi,alivyokata simu tu haraka akatembea mpaka chumbani kwake akamuacha Sonia yupo juu ya meza anatizama huku na kule nayeye akashuka na kuingia chumbani.
“Baby vipi?”
Sonia aliuliza baada ya kumuona Stuwart anavaa nguo akiwa kama amechanganyikiwa.
“Nimepigiwa simu na bosi sasa hivi niwahi ofisini nimechelewa alafu”
“Sasa hata kuoga?”
“Hapana kwa kweli,jiandae nawewe vilevile au unataka kubaki?”
“Akuu,namimi nataka kuwahi chuo”
“Basi vaa chapchap,tuchukuwe bodaboda”
Wote walivaa harakaharaka bila ya kuoga.
“Viatu vyangu viko wapi?”
Sonia alimuuliza Stuwart baada ya kuvaa tayari.
“Achana navyo,vaa hivyo hapo”
Sonia akaingiza mguu ndani ya raba za Stuwat,wote wakatoka nje wakafunga mlango na funguo.
Stuwart alitembea hatua kubwa mpaka nje ambapo kulikuwa na pikipiki nyingi.
“Oyaaa psiiii bodaboda”
Pikipiki ikasogea mpaka miguuni kwao.
“Wapi mkuu?”
“Posta,posta mpya pale mtaa wa samora”
“Elfu kumi”
“Poa”
“Sikia mwite na mwenzako”
Pikipiki nyingine ikasogea miguuni mwa Sonia.
“Hostel Mabibo naenda”
“Kumi na tano”
“sawa”
Stuwart akampatia Sonia pesa na hapo ndipo walipoachana, Pikipiki aliyopanda Stuwart ilielekea Magharibi na Stuwart Mashariki.
Upepo ulimpuliza Sonia akiwa nyuma ya pikipiki ikiwa katika mwendo.
“Kakaaaaa”
Sonia akaita kwa Sauti ili kushindana na upepo mkali.
“Vipi?”
“Utaniacha Mwenge”
“Pale Stendi?”
“Ndio”
“Kwahiyo huendi tena Mabibo Hostel?”
“Wewe niache Mwenge kwenye zile bajaji”
“Hakuna shida”
Bodaboda ilizidi kupita kandokando,wakatokea barabara ya Makumbusho mpaka walipofika Stendi ya Mwenge dereva akasimamisha pikipiki.Sonia akatoa pesa.
“Hapana usijali,baki nayo hiyo chenji”
Sonia aliacha chenji iliyobaki,akatembea mpaka kwenye bajaji na kukodi moja wapo ambayo ilimpeleka mpaka Nyumbani kwake Mikocheni B.Kitu cha kwanza alichofanya ni kumtafuta Alex hewani.
****
“Upo wapi?”
Hilo ndilo swali la kwanza kuuliza Alex tena kwa jazba baada ya kupokea simu kutokea kwa Sonia.
“Nipo home”
Sonia alijibu kwa kujiamini.
“Una uhakika?”
“Alex una nini lakini?”
“Jibu swali”
“Nina uhakika ndio.Nipo nyumbani”
“Mbona ulikuwa hupokei simu zangu?”
“Ilikuwa kwenye chaji”
“Unasema?”
“Simu ilikuwa kwenye chaji”
“Ndiyo ushindwe kupokea al..titititi”
Sonia alikata simu kwa makusudi ili kutingisha kiberiti,alimuelewa sana Alex alivyokuwa dhaifu na alijuwa ni lazima angepiga tu.Ni kweli kama alitabiri vile,Alex akapiga.
“Mbona umekata simu?”
“Nimechoka na maswali yako.Tusiharibiane siku sawa.Nimekujibu maswali yako,sijui unataka kitu gani kingine”
Sonia akajifanya kuongea kwa sauti ya ukali akitaka kupima maji!
“Nisamehe baby,kidogo akili yangu haipo sawa.Nipo kwa Stuwart hapa.Nakuja kwako”
“Sawa karibu”
Kwa jinsi Sonia alivyocheza mchezo huo alijikubali mwenyewe akajipa ‘Big up’ akatembea mpaka bafuni akaoga na kutoka mpaka Seblen ambapo aliingia jikoni na kufungua friji,akatoa soseji tatu akaziweka jikoni akaangalia juu na kutoa mkate akaupaka siagi,alihisi njaa kiasi.
Akaweka maji jikoni yachemke ili anywe chai.Kila kitu kilivyokamilika akaweka mezani na kuanza kujichana mguu mmoja kaukunja juu ya kiti.
***
“Vipi una miadi naye?”
“Askari kwani wewe hunijui mimi?”
“Nakufahamu sana lakini haijalishi,mpaka atoe ruksa”
“Basi kamwambie kuwa Alex nimefika”
Askari aliyekuwa analinda nyumba ya Sonia alikuwa anazozana na Alex,gari yake haikuruhusiwa kuingia ndani ndiyo maana akagoma kufungua geti.Hivyo ndivyo alivyoambiwa na tajiri yake kwamba asipite mtu yoyote yule bila ridhaa yake.
Askari akatembea mpaka mlangoni na kugonga.
“Vipi afande?”
Sonia akauliza baada ya kutoa kichwa chake nje.
“Kuna mtu yupo getini anataka kuingia anaitwa Alex”
“Oh,Mruhusu”
“Sawa Mama”
Mlinzi akatembea na kusukuma geti la kisasa lililokuwa na Matairi madogo chini,Prado la Alex likaingia ndani.
Sonia alilisindikiza kwa Macho mpaka likafika sehemu maalum,likasimama pembeni ya gari lake, Landcruiser Rexas.
“Baby angalia maua yangu,usije ukayakanyaga”
Sonia akaweka utani,Alex akashuka akatembea wote wakakumbatiana.
“Hapana baby sio hapa twende ndani”
Sonia hakutaka kuliwa denda mbele ya walinzi,wakaingia ndani wakaanza kupigana mabusu.
“Karibu chai love wangu”
“Ahsante nishakunywa”
Alex alimtizama Sonia akiwa kama ana kitu anataka kuzungumza naye ama kumuuliza lakini alisita,aliogopa anaweza akamkasirisha na ndiyo maana akakaa kimnya bado alishindwa kuelewa alichoambiwa na Latifah kama ni kweli au ni uzushi.
“Nilikumisi,safari bado siku ngapi?”
“Siku mbili lav,ushapaki?”
“Ndio”
“Beba basi mabegi yako tuondoke,ukakae kwangu”
“Okay love”
Hivyo ndivyo ilivyokuwa,Sonia akaongoza chumbani na alivyotoka alikuwa na begi dogo mkononi mwake.
“Nguo zako zote zipo humo?”
“Kila kitu”
“Haya tuondoke”
Wote wakaongozana na kuingia ndani ya gari,Muda wote Alex alionesha tabasamu.Akageuza gari mlinzi akafungua geti,gari likatoka nje.

****
Kitu cha kwanza walivyofika Sonia aliweka mabegi chumbani na kuanza kunyonyana midomo yao kama njiwa,Alex alikuwa na moto kupita kiasi, kwa Sonia ilikuwa kawaida sababu alitoka kufanya ngono na Stuwart muda mchache uliopita na alikuwa amechoka kiasi.
“Baby”
“Mhhh”
Alex akaitikia kwa kuguna.
“Leo mgongo unaniuma,tufanye baadaye please please”
Sonia alitoa kisingizio.
“Okay love hata hivyo ngoja niende kazini kuna mambo sikuacha vizuri”
“Okay baby”
Alex akaweka shati lake vizuri akatoka nje na kumuacha Sonia chumbani peke yake akielekea ofisini kwake,alimpenda sana Sonia na alikuwa yupo tayari kuoa tena kwa mara nyingine.

****
Baada ya masaa mawili kupita tangu Alex aende kazini nje alisikia mtu akibisha hodi,akiwa seblen amejiachia na sketi fupi ya kimini akainuka na kuufungua mlango.
“Shikamoo”
“Marahaba hujambo binti?”
Mzee mfupi kiasi mnene aliyechomekea suruali mpaka kifuani yaani mayenu, ndiye aliyekuwa mlangoni.
“Sijambo karibu”
“Ahsante,Alex yupo?”
“Ametoka sasa hivi”
Mzee huyo mwenye kitambi aliingia ndani na kutoa simu yake mfukoni,akamtafuta Alex hewani wakati huo Sonia alikuwa kimnya anatizama televisheni.
“Nipo hapa kwako,Marahaba… Eh ndiyo ndiyo sawa hakuna shaka.Usijali”
Mzee huyo aliongea na Simu na upande wa pili,Sonia hakuyasikia mazungumzo hayo lakini alitambua kuwa anaongea na Alex.Mzee akamtizama Sonia,macho yake yakatua juu ya mapaja ya Sonia.Akajikoholesha kidogo.
“Binti unaitwa nani?”
“Rachel”
“Alex upo naye vipi?”
“Ni rafiki yangu.Nimekuja kumuona mara moja”
“Mimi ni baba yake mdogo naitwa Mr.Stanley Mwandambo huyu ni kama mwanangu,tangu marehemu baba yake afariki dunia mimi ndiyo nilikuwa nikimlea,nikamtafutia kazi nzuri.Unaishi wapi?”
Mr.Stanley Mwandambo alianza mazungumzo marefu ambayo hata hakuulizwa huku mara kadhaa macho yake yakiwa juu ya mapaja meupe ya Sonia yaliyokuwa wazi manene,Sonia alilijua hilo ndiyo maana akazidi kupandisha sketi yake juu tena,mzee akazidi kuchanganyikiwa.
“Mimi naishi Kigogo”
Sonia akajibu kwa mapozi.
“Unasoma?”
“Nimemaliza shule natafuta kazi ndiyo maana nipo hapa kwa Alex,kaka yangu ndiyo kaniambia nije kumuona leo.Ninamsubiri”
“Una elimu gani?”
“Form four”
“Usijali,achana na Alex mimi nitakupa kazi nzuri sana Rachel,una simu?”
“Ndio”
“Nipatie namba zako”
Uwongo wa Sonia ulikuwa na PHD na alikuwa yupo siriazi wala hakucheka akatoa namba kwa Mr.Stanley.
“Wacha mimi niende nitakupigia simu,sawa Rachel”
“Kweli utanipa kazi?yaani ukinipa kazi nitakupa chochotre kile unachotaka”
Sonia aliongea kwa kujilegeza na kumfanya Mzee Stanley Mwandambo apagawe kabisa,kwa Sonia ikawa ni kama amerahisishiwa kazi kwani ilikuwa ni lazima asambaze ukimwi na kuumaliza ukoo wa MWANDAMBO!

 Maneno ya Sonia yalizidi kumchanganya Mr.Stanley Mwandambo akazidi kumuangalia binti huyu mdogo asiyekuwa na kasoro kuanzia juu mpaka kwenye unyayo.Aliziangalia nywele zake za singasinga,macho yake makubwa na alivyotuliza macho yake juu ya kifua cha Sonia ndiyo kabisa.Kifua cha Sonia kilikuwa kimechongoka,maziwa yake yamesimama yaani chuchu saa sita na kumfanya mzee huyu adate.
“Leo nitakupigia simu au ngoja nikupigie hapa ili usevu namba zangu”
Siyo kwamba Mr.Stanley Mwandambo alitaka namba yake awe nayo Sonia kwa wakati huo la hasha!alikuwa anataka kuhakikisha kuwa namba alizopewa ni sahihi ama za behewa la treni,hapohapo aliipiga simu ya Sonia iliyokuwa mezani ilianza kuita,akaichukuwa.
“Sasa nikusave vipi?”
Sonia akauliza.
“Chochote tu”
“Sawa”
Mzee Mwandambo akasimama na kuaga mara mbilimbili huku akimtizama Sonia juu ya mapaja yake.
“Nitakupigia,sawa?”
“Ahsante nitashukuru sana”
Hatimaye mzee Mwandambo akaaga na kuondoka zake.
Sonia alibaki akiangalia televisheni akiwa ana waza juu ya maisha yake,alivyokumbuka mimba aliyokuwa nayo tumboni ndiyo ikamchanganya zaidi, swala hilo ndilo likamnyima raha ya maisha,kilichomzindua katika mawazo aliyokuwa nayo ni simu iliyoanza kuita.Akaitizama juu ya kioo na kugundua aliyekuwa anapiga ni Mustapha.
“Halloo Mustapha”
“Sonia,habari za siku nyingi?”
“Nzuri tu”
“Hivi mara ya mwisho kuwasiliana na Nasra ni lini?”
Lilikuwa ni swali alilouliza Mustapha likamfanya Sonia akae kimnya kidogo,hakuelewa ni kitu gani akiseme,sio kwamba hakujua ni wapi mdogo wake alipo lakini alishindwa aanzie wapi kumueleza Mustapha.
“Sonia”
“Abee”
“Nasra una mawasiliano naye?kama una namba zake nyingine anazotumia huko tafadhali naomba unitumie”
“Kwa kweli ni muda mrefu sana sijafanya naye mawasiliano”
“Dustan kesharudi?”
“Aliniambia anarudi tarehe 24 nadhani ni keshokutwa”
“Sawa”
Sonia akakata simu,mawazo yake yakaenda kwa Nasra alimuurumia sana Mustapha na alimsikitikia sana mdogo wake Nasra na kumchukia Sebastian vilevile.Chanzo cha wadogo zake kupata ugonjwa wa Ukimwi kilisababishwa na Sebastian ambaye ndiye yeye alimpa ukimwi,swala hilo lilimuuma sana moyoni.
****
Nasra alikuwa yu uchi wa mnyama nguo zake zipo kandokando na ndiyo hivyo alivyoamriwa,mbele yake walisimama wanaume wanne wenye silaha za moto.Kitendo hicho kilimfanya azidi kuogopa zaidi,mwanaume mmoja mwenye misuli na aliyejazia mkono akamsogelea na kuanza kumuangalia kifuani kwake macho yake yakazidi kushuka chini ambapo Nasra alikuwa ameweka mikono sehemu zake za siri.
“Unaziba ziba nini?toa mikono hiyo”
Jitu hilo likaamru,Nasra kwa hofu akaondoa mikono yake jitu hilo likatabasamu.Sebastian aliyekuwa chini alishuhudia kila kitu akiwa anavuja damu mdomoni nayeye anatetemeka kwa hofu.
“Simama juu”
Ni kauli nyingine ambayo ilitoka na ilimlenga Nasra,katika maisha yake hakuwahi kusimama uchi wa myama mbele ya wanaume wengi kama hivyo.
Alihisi aibu na alitafsiri kitu kama hicho kama udhalilishwaji ingawa hakuelewa nini mwisho wa yote japokuwa akili yake ilimtuma kuwa kitakachofuata hapo ni kuingiliwa kimwili, hakuelewa itakuwaje kama atafanyiwa hivyo na kundi la watu,alivyoyafikiria hayo alianza kulia machozi.
“Simama juu nimesema”
Nasra akasimama kinyonge,jambazi akamzunguka akawa anamkaguwa nyuma.
“She is clean”
Kauli hiyo ilivyotoka tu akaamriwa akae kando,akaletewa nguo nyingine za kijani avae.
“Vipi kuhusu huyu Sebastian?”
Jambazi mwingine akauliza.
“Unahisi atahitajika sana?”
“Sidhani”
“Kwahiyo?”
“Unajua maana yake”
“Tumuuwe?”
“Ndio”
Majambazi yaliteta pembeni walionekana walikuwa na mpango kabambe ambao walitakiwa kumtumia Nasra.Kwa maana hiyo hawakuwa na haja na Sebastian.
“Au tusimuuwe anaweza akasaidia mbele nishakumbuka”
“Kweli?”
“Ndio”
“Aya kafanye mipango”
Baada ya kuteta wakamsogelea Sebastian na kumuamuru nayeye pia avue nguo zake zote azitupe kando.
“Ebwana usitupotezee muda wetu”
Mapigo ya moyo ya Sebastian yalipiga kwa nguvu hakuelewa hasa kitu gani watu hao wanataka,walikuwa ni marafiki zake ambao alishirikiana nao katika matumizi hatari ya madawa ya kulevya lakini siku hiyo walimbadilikia kuliko kawaida.
“Kwanini mnafanya hivi?”
“Usituulize maswali Sebastian,vua nguo”
Akavua nguo zake zote,nayeye akakaguliwa akapewa nguo nyingine avae.

Baada ya hapo wakafungwa kamba kwa nyuma na kuvalishwa vitambaa vyeusi usoni.
Wakachukuliwa na kuingizwa ndani ya gari hapohapo gari likawashwa safari ikaanza.
Hakuelewa ni sehemu gani wanaenda sababu ya vitambaa vyeusi vilivyokuwa usoni mwao. Ulikuwa ni mwendo wa kama kilomita arobaini na sita sababu gari lilitembea kwa muda mrefu,Sebastian alijua kivyovyote vile walikuwa tayari wametoka nje ya mji.Na baada ya dakika ishirini gari likasimama akahisi mlango unafunguliwa,wakashushwa ndani ya gari.
“Tuku tuku tuku tuku”
Ulikuwa ni mlio wa Helkopta uliokuwa unasikika kwa mbali,kutokana na kufunikwa na vitambaa vyeusi hawakuelewa kuwa wapo katika fukwe za bahari .
Lakini walisikia mlio huo wa helkopta,huku michanga ikiwa inaruka,helkopta iliyokuwa inazungusha mapanga boi ikatua ardhini wakashuka wanaume wawili wenye ndevu nyingi usoni,kwa harakaharaka hawakuwa wamarekani,walikuwa ni waarabu lakini rubani alikuwa ni mzungu.
Hakukuwa na mazungumzo zaidi ya kuwapakia Sebastian na Nasra ndani ya helkopta kisha majambazi wote wakaingia,Helkopta taratibu ikaanza kuinuka juu na kugeuka na kuondoka ikazidi kupanda juu angani.Sebastian na Nasra walizidi kuchanganyikiwa kupita kiasi.
Na Helkopta ilivyokuwa angani mara nyingi walisikia lugha ya kiarabu kwa maana hiyo hawakuelewa nini kilichokuwa kinazungumziwa.
“Salim,tunakaribia kufika kisiwani.Utashusha ndege pale”
“Sawa”
“Mahmoud ndiye atakupeleka kwenye ngome huko tutasafiri tena”
“Sawa hakuna shida,kwahiyo tunaondoka leoleo?”
“Ndio,lazima tufike leo ili tumfurahishe tajiri Yusuph”
“sawa”
Rubani aliyefahamika kwa jina la Salim alikuwa akiongea na mwenzake,wote walikuwa wamevaa mitambo maalumu iliyofanana na ‘headphone’ za ma dj,hizo ndizo walizotumia ili wasikilizane.Helkopta ikazidi kusonga mbele na taratibu kuanza kushuka chini baada ya kuona kisiwa.
Ilivyotua tu wakatokeza watu wengine,waliofunga vitambaa vichwani,kutokana na ndevu zao ilionekana dhahiri walikuwa waarabu.
“Asaalam Aelukuy”
“Waalekuy Mslam”
Hizo ndizo salamu walizotumia kusabahiana huku wakikumbatiana,Sebastian na Nasra wakashushwa, bado walikuwa na vitambaa vyeusi usoni na hawakuelewa wapo wapi na wakina nani, walichosikia ni lugha ya kiarabu.
“Boti zinatusuburi huku,twendeni haraka hakuna kupoteza muda”
“Chukuwa hao watu,twendeni upesi”
Safari ilianza upya,Nasra na Sebastian wakapakiwa kwenye boti ndogo ya mwendokasi.Injini ikawashwa wakasonga mbele,ilikuwa ni safari ndefu na iliyowatia mashaka.
****
“This is the message to Americans,I’m going to cut his head off now.Allah Akbar”(Huu ni ujumbe kwa Wamarekani,naenda kukikata kichwa chake)
Ilikuwa ni katikati ya usiku wa saa saba,video hiyo iliachiwa mitandaoni na kufika moja kwa moja ikulu ya Marekani.Mwarabu aliyejifunika uso wake alikuwa ameshika kisu kirefu na chini mwanaume wa kizungu kapigishwa magoti kisu kipo shingoni mwake.Ilikuwa ni picha ya kutisha kwa Raisi wa Marekani Barack Obama,alishaelewa nini maana ya watu wake kuchinjwa.Kilikuwa ni kisasi kutoka kwa Mtoto wa Osama Bin Laden aliyeitwa Yusupuh Bin Laden.Kitendo cha wamarekani kumuua Osama Bin Laden kilimfanya mwanaye alimbikize kisasi kwa kuwachinja raia wa Marekani na kuwauwa,alifanikiwa kutengeneza mtandao mkubwa sana ndani na nje ya nchi,akawa ana mawakala wake waliotapakaa karibia dunia nzima.
Raisi Obama,alishuhudia mtu akichinjiwa kupitia kioo kikubwa,pembeni kulikuwa na wazee wengine wa kimarekani wanatizama,wengine waliweka mikono yao kichwani wengine midomoni.Picha hiyo ilitisha mno,kichwa na Mmarekani mwenzao kilikuwa chini kinavuja damu kimetenganishwa na kiwiliwili.
Na huko ndipo Sebastian na Nasra ilibidi wapelekwe ili wachinjwe na Yusuph Bin Laden.
*****
Sonia na Alex Mwandambo waliingia nchini Uganda katika uwanja wa kimataifa Entebbe airport na shirika la ndege ya RwandAir saa moja ya jioni,mji ulikuwa una hekaheka kuliko kawaida.
Muda wote Alex alikuwa nyuma ya Sonia tena kaitanua mikono yake.Uzuri wa Sonia ulimchanganya na ndiyo maana alitaka amfanye afurahi katika maisha yake yote,ni kweli alimpenda mwanamke huyo na kuamini kama yeye ni chanda basi Sonia ni pete ingawa alikuwa ameoa hilo hakulijali sana,hawakuwa na mizigo mingi kila mtu alikuwa na begi dogo ambapo walitoka nje ya lango la uwanja wa ndege na kutafuta taxi.
“Sebbo jebaleko”(Habari yako mkuu)
Dereva taxi alimuongelesha mteja wake na kumchangamkia.
“I don’t speak your language”(Sijui lugha yenu)
Alex akajibu.
“Kale nawe jeballe”(Nzuri tu)
Sonia alidakia na kujibu lugha ya kiganda hiyo ilimfanya Alex ashtuke na kumgeukia.
“Unajua kiganda?”
“Kidogo sana”
“Ulikijulia wapi?”
“Niliwahi kusoma huku”
“Hukuwahi kuniambia”
“Nilifukuzwa shule,any way nimechoka baby ni stori ndefu”
Alex akamgeukia dereva taxi na kumuagiza awapeleke Hotel iliyoitwa HBT iliyokuwa jijini Kampala nje ya mji huo wa Entebe kama kilomita sabini.
Wote wakaingia ndani ya taxi viti vya nyuma na safari ikaanza.Sonia alikumbuka vitu vingi sana.Nchi hiyo ilimkumbusha matukio mbalimbali kupita kiasi,vitu vingi vikawa vinapita ndani ya akili yake,akamkumbuka Partson kipindi wanasoma shule jinsi walivyokutana.
Lisaa limoja na nusu waliingia mjini Kampala dereva akakunja barabara ya Namirembe akalipita jengo la Mukwano Mall mbele kidogo akaweka gari kando.
“Tumefika Sonia”
Alex na Sonia wakashuka,wakamlipa dereva ujira wake.
“Huku umepajuaje Alex?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Sonia.
“Nilishawahi kufanya kazi huku miaka kama miwili iliyopita,nilikuwa nafikia katika hii hoteli.Lakini hii nchi ninaiogopa sana”
“Kwanini?”
“Wanasema kuwa ugonjwa wa Ukimwi ndio upo huku,asilimia tisini ya waganda wana ngoma”
Sonia alimtizama Alex kwa kitambo kidogo,alimsikitikia sana sababu kitu anachokiogopa tayari alikuwa nacho mwilini.
“Kitu ninachokiogopa katika maisha yangu ni UKIMWI Hafuan”
Alex alizidi kuongea bila kujua lolote,walifika mapokezi huku Sonia akiwa kimya bado.
Waliandikisha majina yao na kupewa funguo.

Kabla ya kufanya chochote walivua nguo zao na kupita moja kwa moja bafuni sababu chumba walichopewa kilikuwa ni ‘self contained’.Huko ndipo walipoanza kunyonyana ndimi wakiwa wapo uchi wa mnyama maji ya mvua yanawamwagikia,kwa Alex alimuona Sonia mpya kila kukicha na wala hakumchoka kabisa,aliona yupo sahihi kumuacha mke wake na kuwa na Sonia kimapenzi wala hakujuta hata kidogo.Walishikana shikana kila sehemu ya miili yao,ndizi ya Alex ilikuwa tayari ipo wima na Sonia alikuwa anaichua taratibu na mikono yake laini hiyo ikamfanya Alex azidi kupagawa zaidi na zaidi,midadi ilivyompanda akamvuta Sonia na kumtoa bafuni akamtupa kitandani puu,wakaendelea kulana denda.Hapo akashindwa kuendelea ilibidi aikamate miguu ya Sonia akaipanua huku na kule akaingiza ndizi yake ndani ya mgodi wakaanza kufanya mapenzi,Alex alishakuwa MTUMWA WA NGONO tayari.Hakuelewa kuwa tayari hapo alipo damu yake ina vidudu hatari wa virusi vya ukimwi.
***
“MREMBO UPO WAPI?MBONA SIMU YAKO HAIPATIKANI?”
“NIPO MBONA LAKINI NIMESAFIRI KIDOGO NIPO RWANDA”
“RWANDA?”
“NDIYO,KWA MJOMBA NIMEKUJA KUMUONA ANAUMWA”
“SASA HATA KUAGA LOVE,UNARUDI LINI?”
“SIJAJUA LAKINI NADHANI NEXT WEEK”
Sonia alikuwa simuni akichat katika mtandao wa 'WatsApp'na Stuwart tena pembeni yake alikuwa amelala Alex.Akaingia kwenye namba nyingine akakumbana na Meseji ya Mr.Alex Mwandambo.
“RACHEL VIPI?DP YAKO NZURI”
“THANKS”
Alijibu,akasubiri kidogo akaona imeweka tiki mbili,mara akaona Mr.Alex yupo Online tena akiwa anaandika ujumbe.
“UPO WAPI NISHAKUTAFUTIA KAZI”
“AHSANTE SANA,NIJE KUANZA LINI?”
“HATA LEO,NITUMIE BASI PICHA ZAKO HATA MBILI RACHEL.ZILE NZURI NZURI”
“OKAY”
Japokuwa Mr.Stanley Mwandambo alikuwa mzee lakini alikuwa ana mambo fulani ya kihuni,Sonia alilijuwa hilo nayeye alitaka kumpeleka kihuni vilevile.
Alikuwa amevaa kanga moja peke yake asubuhi hiyo,akaiweka kihasara akajipiga ‘selfie’ na kumtumia Mzee Stanley Mwandambo.
***
Picha ya Sonia ilimvuruga sana akiwa ofisini kwake,mapaja ya mwanamke huyo yalimchanganya akilli yake akahisi mwili wake unasisimka mno.Hakutaka kuvumilia, hapohapo akafungua mkanda wake na kushusha suruali chini,akatema mate juu kiganja chake cha mkononi akashika koki yake vizuri huku akiitizama picha ya Sonia iliyokuwa juu ya simu yake akaanza kuvuta hisia na kuanza kujichua,akamvua nguo Sonia akayafumba macho yake huku akizidi kujichuwa mwenyewe.Akawa anafanya ngono na Sonia kihisia,akili yake yote ikahama kabisa akajisahau kama yupo ofisini.Kila sekunde zilivyozidi kwenda mbele ndipo alipozidi kuhisi raha za ajabu,akaanza kuhema ndani kwa ndani.Hapohapo risasi zikaruka na kuchafua meza yake,alivyoyafumbua macho yake hakuamini.Alidhani yupo ndotoni.Mbele yake alisimama mwanaye, Stuwart.
“Stuw stuwart st…uwart”
Stanley Mwandambo alijisikia aibu vibaya sana,akashindwa ni kitu gani akiseme mbele ya mwanaye wa kiume, Stuwart.

 Kitu kilichotokea bado aliendelea kudhani ni kiini macho,aibu iliyomshika haikuwa na mfano wake.Mashine yake ilikuwa nje bado tena ina uteute akaishiwa pozi kabisa.Akabaki anamwangalia mwanaye Stuwart aliyekuwa mbele yake ameduwaa haamini kuwa huyu ndiye baba yake.Kwa kuwa alimuheshimu hakutaka kuuliza kitu chochote kile,akainamisha kichwa chake na kutoka nje.Bado Mr.Stanley alihisi haya ajabu.Kitu alichokifanya kilikuwa cha kipuuzi na kwa umri kama wake tena akiwa ofisini mwake, akajizoa zoa na kufunga zipu yake kisha kuketi juu ya kiti.
***
“Ndio ndio,Nipo HBT Hotel.Kwahiyo ni leo au?”
Alex alikuwa simuni anazungumza na mtu upande wa pili wa simu, ilielekea ndiyo hao waliomfanya afunge safari kutoka Tanzania Mpaka nchini Uganda.
Pembeni kulikuwa na Mwanamke mrembo amevaa kanga peke yake,mwenye macho makubwa mazuri ya duara,anamuangalia kwa kila sentensi anayoongea hakuwa mwingine bali ni Sonia Nickson Shayo.
“Bab...”
“Subiri nimalize kuongea na simu”
Sonia alikatishwa na Alex,alipomaliza kuongea na simu akamgeukia Sonia.
“Vipi Hafuan?”
“Nimekumisi”
“Nipo hapa mbona”
Kwa akili ya ki utu uzima aliyokuwa nayo Alex alielewa nini maana ya sentensi hiyo lakini alivyojaribu kumvuta Sonia karibu ili amnyonye lips ikashindikana Sonia akakwepesha mdomo wake,kumaanisha kuwa hakuwa tayari kufanya tendo hilo kwa wakati huo.
“Vipi?”
“Hakuna kitu,nipo period”
“Imeanza lini?”
“Jana usiku”
Sonia alikuwa ni muongo sababu hakuwa tayari kufanya tendo hilo,alihisi mwili wake hauna nguvu na hakuelewa ni kitu gani kinasababisha jambo hilo lakini ghafla akagundua kitu kinachomsumbua ni mimba changa,alihisi baridi na kichefuchefu.
“Nakuja love”
Sonia akasimama kutoka kitandani na kuingia bafuni.Huko ndipo alikimbilia sink na kuanza kutapika,alibanwa na kichefuchefu kikali cha kutapika,mwili wake ulikuwa unatetemeka ajabu.Alex akasogea na kumfuata nyuma yake.
“Tatizo nini?”
“Nothing”
“Mbona unatapika,unaumwa?”
Sonia hakujibu swali hilo lingine japokuwa alilisikia.
“Hafuan,una shida gani?”
“I said nothing”(Nimesema sio kitu)
Hakuwa tayari kuongea lolote kuhusiana na mimba aliyokuwa nayo kwa sababu aliichukia mno na jinsi Alex alivyokuwa anamuuliza maswali alihisi kichefuchefu zaidi.
“Hafua…”
“Nimekwambia sio kitu siumwi,niache Alex”
Sonia alipayuka kwa sauti ya juu iliyosindikizwa na ukali juu yake,akamkata Alex jicho kali sana na kumfanya aogope.
“I’m sorry”
Hivyo ndivyo alivyosema Alex,japokuwa hakuelewa ni kosa gani alilolifanya.Hakutaka kumuudhi Sonia ndiyo maana akaomba radhi.
“Nataka kurudi Tanzania”
“Hafuani lak..”
“Nadhani Umenisikia,nataka kurudi leo”
Alex ndiye alikuwa akiambiwa maneno hayo na Sonia,ni kweli mwanaume huyu mtu mzima aliburuzwa kama mtoto mdogo,alipanga wafike nchini Uganda wafurahi na kusherekea baada ya kikao lakini ghafla Sonia alibadili mawazo.
“Ngoja basi kikao kiishe tutarudi”
“Sitaki”
Hakukuwa na punje ya masihara hata kidogo ndani ya maneno ya Sonia,sababu alianza kutembea mpaka kabatini na kuanza kuchukuwa nguo zake.
Hilo ndilo likamfanya Alex agundue kuwa mwanamke huyo afanyi masihara na alimuelewa vizuri Sonia kwamba akishaamua kufanya kitu haikuwa rahisi kumbadilisha mawazo.Na ndicho kilichotokea.
“Subiri basi nipige simu ni cancel mkutano”
“Endelea na mkutano.Mimi naondoka mwenyewe”
“Hafuan please,usinifanyie hivyo”
Chumba nambari 305 ndani ya hotel ya HBT ndiyo kilichokuwa kimepangishwa Sonia na Alex na daftari liliandikwa kuwa watu hao wangekaa kwa muda wa wiki tatu lakini mambo yalibadilika Sonia alitaka kuondoka baada ya siku hiyo moja tu,hiyo ilimpagawisha sana Mr.Alex Mwandambo.
Akashindwa ni kitu gani akifanye kwa wakati huo sababu alimpenda sana Sonia kutoka ndani ya moyo wake.
“Nimeshaamua”
Hivyo ndivyo ilivyokuwa, Sonia akaweka kila kitu sawa,akavaa begi lake mgongoni.
“Nisubiri tuondoke wote”
“Sawa”
Haikuwa kwa matakwa yake bali kwa nguvu ya penzi na ilielekea kuwa Alex Mwandambo kwa Sonia alikuwa hapindui hata kidogo na kama angekuwa ni muislamu basi Alex alikuwa tayari kumuoa Sonia,dini ya kikristo ilipinga kuoa wake wawili na ndiyo maana Alex akashindwa kufanya hivyo.
Walitoka chumbani na kukabidhi funguo kwa msichana mdogo aliyekuwa mapokezi kisha kutafuta taxi.
Ndani ya gari Sonia hakuongea chochote alikuwa amenuna kupita kiasi.
“Ongea basi baby,tatizo nini?”
Lilikuwa ni swali lingine kutoka kwa Alex lakini yeye aliendelea kukaa kimnya,mimba ilikuwa ikimchanganya mbaya zaidi aliichukia,kichwani mwake alitafakari ni kwa njia gani ataweza kuilea na kama mtoto angezaliwa alijua kabisa angepata ugonjwa wa ukimwi kutoka kwake,alisikitika sana kuuwa kiumbe kisichokuwa na hatia.Hayo ndiyo yalikuwa yakimiminika kichwani kwa Sonia siku hiyo.
“Hafuaaan…”
“Alex embu naiache tafadhali,kuanzia leo tusijuane”
Kitu kama hicho Alex alikichukulia kama utani ndiyo maana akabaki anamtizama Sonia na kutabasamu.
“Acha masihara basi”
“Nipo Siriaz naomba tuachane”
“Kwanini?”
“Nimeamua tu”
“Haf…”
“Alex naomba nielewe,sikutaki tena”
Kama mapenzi na mahitaji yote alipewa ndiyo maana hata Alex akashindwa kuelewa ni kosa gani kalitenda,akamuangalia Sonia bila kummaliza haikuwezekana hata kidogo mambo yawe ghafla kiasi hicho.
“Hafuan,nini tena kimekupata?”
“Sio kitu”
“Kumbe?”
“Ni maamuzi”
Dereva taxi aliendesha gari lakini masikio yake yalikuwa waluwalu,mara kadhaa alikuwa akiangalia kioo cha katikati.Hakuelewa Kiswahili lakini alijuwa kivyovyote vile wateja wake wana tatizo lakini hakutaka kuuliza swali sababu aliamini kuwa hayamuhusu.
“Hafuan embu usiniletee upuuzi”
“Unasemaje Alex?”
“Usiniletee upuuzi,nimemuacha mke wangu nimekatisha kikao unajua mamilioni ngapi ya pesa nimepoteza eeh?unajua ma milioni ngapi ya pesa nimeacha kwenye hicho kikao?”
“Kwahiyo,unatakaje labda?nitajie shilingi ngapi nikulipe….Sebbo stop the car”
Ndani ya taxi hakukuwa tena na maelewano hata kidogo,Alex alipandisha hasira Sonia ndiyo usiseme.
“Driver i said stop the car”(Dereva nimekwambia simamisha gari)
Sonia alifoka na kusisitiza kuwa dereva asimamishe gari,dereva akageuka alivyotaka kuweka gari kando Alex akamkataza.
“You drive,don’t stop”(Endesha gari)
“Stop the car”(Simamisha gari)
“No don’t”(Hapana)
Hakuna siku ambayo dereva taxi alikuwa katika wakati mgumu kama siku hiyo asubuhi,alikuwa mara aweke mguu kati mara aendeleee na safari, wateja wake walimchanganya akabaki njia panda.
“Nipatieni pesa yangu kwanza”
Dereva alihisi wenda baadaye atatoswa na asipatiwe pesa yake, vurugu iliyoendelea ndani ya gari lake ilimtisha,Sonia alipiga kelele kama mwehu.
“Alex niacheeeeeeeee,fuc** you..i said fuc* you Al…”
“Paaaaaa”
Kibao ndicho kilichomnyamazisha Sonia,katika maisha yake Alex hakuwahi kufanyiwa dharau kiasi hicho ndiyo maana akarusha kofi, lililompata Sonia shavuni akajigonga kwenye kioo hapo ndipo alijua ni kweli Alex amekasirika.
“Alex umenipiga?”
“Nyamaza mpumbavu wewe,Keep quit.Kama unataka kushuka ndani ya gari shuka sasa hivi.Driver park the car”
Kilichokuwa kinamuongoza Alex ni hasira zake chafu,alipandwa na hasira na alikuwa yupo radhi kufanya chochote kile kitakacho mtuma.
“Driver,have you heard me?”(Dereva umenisikia)
Hali aliyokuwa nayo Alex ilimtisha dereva akawasha endiketa ya kushoto na kutizama ‘site mirror’ akasubiri mpaka pikipiki ipite akaweka gari kando,barabara ya Enatebe road sehemu iliyoitwa Zana.
“Shuka basi”
Sonia ndiye aliyeambiwa,kwa upande wake hakutegemea kama mambo yangekuwa kama hayo, Alex alikuwa kama mbogo macho yake yamebadililka rangi amekunja ndita kifua chake kinapanda juu na kushuka,meno yake anayabana akawa anamtizama Sonia kama Simba aliyejeruhiwa na mkuki kwenye mbavu,hakuwahi kukasirika kama siku hizo.
“Si unataka kushuka,shuka basi”
Sonia akabaki kimnya,ameinamisha kichwa chini, kiberiti alichokuwa anatingisha kilikuwa kina njiti ndiyo maana akawa kimnya na hakutaka kushuka sababu hakuelewa ni wapi aende.
“Boss”
Baada ya kukaa kama dakika tano nzima ilibidi dereva azungumze,kupaki gari pembeni kulimaanisha pesa kuongezeka na ndiyo maana ilibidi aulize.
“Entebbe airport,let’s go”
Alex akasema na gari likaanza kuondoka,ndani ya gari hakukuwa na maongezi yoyote yale walichuniana na hakuna hata mtu mmoja aliyemuongelesha mwenzake.Sonia alinuna na muda wote aliangalia dirishani.
Mpaka wanafika uwanja wa ndege na kubeba mizigo yao hakuna hata mmoja aliyemuongelesha mwenzake,wakatembea lakini dereva taxi aliwafuata nyuma alionekana kama alikuwa amesahau kitu.
“Mkuu”
“Vipi?”
“Pesa hujanipa”
“Oh samahani”
Alex aliingiza mkono nyuma mfukoni mwake akatoa wallet,akamkabidhi dereva ujira wake na safari ikaanza ya kutembea.Sonia alikuwa tayari katangulia hatua kama ishirini mbele.
“Tukate tiketi business class au?”
Alex akauliza.
“Sijui”
Bado alikuwa amenuna ndiyo maana akajibu kifupi namna hiyo.
Alex akatembea mpaka sehemu maalum ili kuulizia tiketi za siku hiyo na bahati nzuri ilikuwa kwao.

Walipata ndege ya shirika la Uganda inayoondoka saa saba ya mchana,hapo hapo wakatoa passport zao ili zikaguliwe.Wakapewa tiketi na kilichokuwa kinasuburiwa hapo ni Ndege ya Shirika la Uganda,Air Uganda iliyokuwa Zambia,inachukuwa abiria wengine.Huo ndiyo muda wa Alex aliopata kumuongelesha Sonia.
“Hafuan”
“Shida?”
“Leo nikifika kuna cheki inatoka nitakupa milioni mbili”
Alex alijaribu kum-bembeleza Sonia kwa kutumia gia ya pesa,ili kumsahaulisha kila kitu kilichotokea.
“Kwani nimekwambia nina shida na pesa?”
“Hapana nimeamua tu kukupa”
“Sitaki”
“Hafuan sikiliza nikwambie,zile ni hasira hata ungekuwa wewe ni mimi unadhani ungefanya nini?”
Kuanzia hapo Sonia hakujibu kitu aligeuka pembeni na kutoa simu akijifanya kuchati,Alex alimkera kupita kiasi na kwake alichukulia hiyo ni kama dharau.
Kipaza sauti kilisikika ilivyofika saa saba kasoro kuwa ndege ya shirika la Uganda tayari imekanyaga ardhi ya Entebbe hivyo abiria wote walitakiwa waanze kujiandaa,Sonia ndiye alikuwa wa kwanza kusimama akimuacha Alex juu ya benchi,masaa yalizidi kusonga mbele kila hatua ya ukaguzi ilivyokamilika,waliingia ndani ya ndege.Alex aliendelea kutia gia zake lakini Sonia alizipangua hakutaka kumsemesha Alex hata kidogo,bado kichwani aliwaza mambo mengi mno.
“Mbona unakuwa hivyo?geukia huku basi,Nakuomba tafadhali”
“Kwani unataka nini?”
“Ugeukie huku”
“Ili iweje sasa?”
Bado Sonia aliweka ngumu,hakutaka kuelewa somo.Hata hivyo kazi yake ilikuwa tayari imekamilika ya kumteka moyo wake na kumuambukiza ukimwi,Sonia alikuwa ana mambo mawili katika maisha yake, kumuumiza mtu kihisia na kumuambukiza ukimwi.Ndege ilikuwa bado angani inachana mawingu na Alex aliendelea kumuimbisha Sonia lakini wapi!Masaa matatu baadaye sauti nyororo ilitokea kwenye kipaza sauti ikitangaza kwa lugha tofauti tofauti kwamba abiria wote wafunge mikanda, ili kuhakikisha hilo walianza kumkagua abiria mmoja baada ya mwingine.
“Dada funga mkanda”
“Ahsante”
Sonia ndiye hakusikia maagizo hayo sababu alikuwa mbali kimawazo,badaa ya kufunga mkanda,ndege ilianza kuelekezea kichwa chake chini marubani waliokuwa ndani ya chumba chao maalumu wamevaa mashati meupe walianza kufanya mawasiliano na wakaruhusiwa kuishusha uwanja wa kimataifa mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam.
Ikaanza kupiga kelele, ilivyotua ilitingishika na kukaa sawa,ikatembea kwa mwendo wa risasi kisha kupunguza mwendo na kusimama kabisa.
*****
Sonia na Alex walitoka langoni bado wakiwa hawaongeleshani na Sonia akaanza kuchukuwa njia yake.
“Hafuan unaenda wapi?”
Alex aliuliza.
“Kwangu”
“Sasa la…”
Sonia aliendelea kuondoka akimuacha Alex nyuma anamuita,akaingia ndani ya taxi na kuamuru waondoke mara moja.
“Mikocheni B”
“Sehemu gani?”
“Karibu na kanisa la Rwakatare”
“Poa themanini pale”
“Nitakupa twende”
Taxi maalum ya uwanja wa ndege ilikuwa getini tayari na safari ikaanza hapohapo.Aliweka laini yake ya TIGO meseji zisizo na idadi zilimiminika na hapo hapo akapigiwa simu kutoka kwa Stuwart.
“Ulijuaje kama nimeingia Tanzania?”
“Simu yangu imeonesha meseji Delivery sasa hivi,upo wapi?”
“Ndio nipo Airpot hapa natoka nimepigiwa simu na CR kuna pepa ndiyo maana nimerudi”
“Njoo basi K.Nyama”
“Upo nyumbani?”
“Hapana,nipo kazini”
“Home yupo nani?”
“Hakuna mtu funguo nimeacha juu ya mlango wa mbele”
“Poa,utanikuta”
Baada ya simu kukatika Sonia alibadili mahali pa kwenda,hakutaka tena kurudi kwake Mikocheni alitaka akaonane na Stuwart na hivyo ndivyo alivyomwambia dereva wa taxi.

Hakukuwa na namna yoyote ya kumbishia tajiri yake.Dakika arobaini na tano baadaye walikuwa nje ya ukuta mfupi maeneo ya kijitonyama na Sonia akashuka baada ya kulipa pesa, kama alivyoagizwa ndivyo alivyofanya alichukuwa funguo juu ya mlango na kuingia ndani,moja kwa moja akaingia bafuni kujimwagia maji.Akavaa nguo na kurudi seblen.
Kabla ya kukaa sawa alisikia mlango unagongwa akajua tayari Stuwart kafika, kwa mbwembwe za kimahaba na kutaka kumpagawisha akarudi chumbani akavua nguo zake na kuvaa kanga moja peke yake,ambayo iliishia juu ya magoti.Akatembea mpaka seblen na kufungua mlango.Hakuamini alichokiona moyo wake ukaanza kupiga kwa kasi,haikuwezekana hata kidogo kukubaliana na macho yake kwa mtu aliyemuona mbele yake.
“Hafuan”
Alex Mwandambo alipigwa na bumbuazi la waziwazi baada ya kumuona Sonia nyumbani kwa ndugu yake Stuwart tena kavaa kanga tu.


 Bado hakutaka kuamini kuwa mapendo yote aliyompa Sonia ilikuwa ni kazi bure sababu hakuelewa ni kosa gani haswa alilolifanya,alishamfukuza mke wake na kuwatukana wakwe zake kisa mwanamke huyu Sonia aliyedhani kuwa ndiye wake wa kufa na kuzikana,ndiyo maana moyo wake ukamuuma na maumivu aliyohisi hayakuwa na kipimo chake.
Kwa mapendo yote aliyompa yalikuwa ni kama kioo sababu alikuwa akiyaona kichwani,vitu vingi alifikatisha.Akiwa ndani ya taxi anamuwaza Sonia baada ya kuachana uwanja wa ndege, ghafla mawazo yakamjia kuwa aende nyumbani kwa Sonia Mikocheni B akiamini huko angemkuta na wasuluishe kila kitu,huko ndipo aliamini Sonia angefika baada ya kumtibua,alijuta kumpiga kofi na alizilaumu hasira zake.
“Dereva hivi nilikwambia Mikocheni B?”
“Ndio uliniamabia Kwa Mama Rwakatare”
“Hakuna njia yoyote ile ya panya maana sitaki kuchelewa”
“Labda tupitie ya Quality center,tukazunguke K.koo”
“Sio kwamba utazunguka sana?”
“Hapana kaka,kuna njia nitapasua pale katikati huku kuna foleni”
“Aya ilimradi tuwahi”
Dereva ndiye alikuwa akipokea maelekezo kutoka kwa tajiri yake,kilichotokea hapo ni kunyoosha moja kwa moja badala ya kutumia Mandela Road,kichwa cha Alex hakikujaa kitu kingine zaidi ya Sonia kutawala.
Aliwaza ni jinsi gani ya kumuingia mwanamke huyo.

Kwa muda wa kama dakika sitini na nane walikuwa nje ya geti kubwa la kishua hapo ndipo dereva alipoambiwa asimamishe gari na kupewa ujira wake sababu walikuwa wamefika nje ya nyumba ya Sonia.Alex hakuwa na uhakika kama angeweza kuruhusiwa kuingia ndani ya nyumba na walinzi wa Sonia, hilo alilijua kwa asilimia mia moja lakini hakutaka kubadili mawazo yake,akatembea kwa kama hatua tatu na kubonyeza kengele.Akasubiri tena, hapo ndipo alipoanza kusikia parakacha za mtu zinasogea,kidirisha kikafunguliwa sura ya mlinzi ikaonekana.
“Habari afande?”
Mzee Alex alianza kutoa salamu huku akijichekesha lakini askari hakutaka kuonyesha mazoea ndiyo maana aliitikia bila kukenua meno.
“Nzuri”
“Nimemkuta Mama?”
“Hayupo”
“Askari,naomba nipite ndugu yangu najua yupo lakini tafadhali ni muhimu sana”
Maneno ya Alex yalimshangaza askari na aliyachukulia kama kashfa, sababu tajiri yake hakuwepo ndani.
“Nimekwambia hayupo”
“Askari mwambie kuwa nina jambo muhimu mwambie ni Alex najua kuwa amekwambia usinifungulie geti”
Askari alivyoona hivyo ilibidi afungue mlango mdogo wa geti na kutoka nje.
“Hayupo ndani,tusipotezeana muda embu heshimu kazi za watu.Mtafute kwenye simu yake”
“Sawa Ahsante”
Alex hakutaka kuwa mbishi ingawa fikra zake zilimtuma kuwa Sonia yupo ndani lakini hakuwa tayari kuonana naye.Akageuka nyuma na kuita pikipiki iliyokuwa inapita.
“Nipeleke kijitonyama”
“Sehemu gani?”
“Tukifika pale kituoni nitakuelekeza”
“Poa twende”
Alex alipanda nyuma ya pikipiki na safari ya kwenda kijitonyama kuanza mara moja huku akiwa mwenye mawazo tele kichwani.
Alimuwaza Sonia kila wakati na safari ya kwenda kijitonyama ilikuwa kwenda kuonana na ndugu yake Stuwart japokuwa hakuelewa anaenda kufanya nini lakini alijisikia kwenda kuonana naye.
“Sijui nitamkuta,namimi nakuwaje mswahili inakuwaje naenda kwake bila kupiga simu.Anyway nitajua hukohuko”
Alex aliwaza huku akipigwa na upepo uliotokana na mwendo wa pikipiki,alivyofika Kijitonyama kituoni kazi yake ikaanza ya kumuelekeza dereva wa pikipiki mpaka walipofika nje ya ukuta mfupi, nyumbani kwa Stuwart.
“Shika hii”
Alex alimkabidhi dereva ujira wake na kuanza kuingia ndani.Akafika mpaka mlangoni na kugonga akitaka kujaribu kama kweli Stuwart yupo, kilichompa moyo ni kusikia sauti ya televisheni,akagonga tena mlango.Hatimaye akasikia kitasa kinanyongwa baada ya dakika tano kupita.Jinsi alivyoyatumbua macho yake ilitisha hakutofautishwa na mtu aliyepoteza nauli ndani ya daladala.
“Hafu..an”
Hivyo ndivyo alivyosema Alex huku akiwa amepigwa na butwaa lisilokuwa na kipimo chake.Isingewezekana hata kidogo kwa kitu alichokishuhudia kiwe cha ukweli.
“Unasemaje Alex?”
Sonia akajibu kwa ujasiri hiyo ndiyo ikamchanganya Alex kwa kiasi cha kutosha, mapigo yake ya moyo aliyahisi yamesimama kwa muda na damu haitembei,alihisi kupalalaizi mwili mzima.
“Una una..unafanya nini hapa?”
Lilikuwa ni swali ambalo jibu lake lilikuwa wazi kabisa kutokana na picha iliyokuwa mbele yake, kutokana na presha akajikuta anauliza swali hilo bila kutegemea.
“Mimi ndiyo natakiwa kukuuliza unafanya nini hapa?”
“Hapa ni kwa ndugu yangu”
“Namimi hapa ni kwa…..”
Kabla ya kumalizia anachotaka kuongea,Sonia akatupa macho yake getini na kumuona Stuwart anaingia.
“Baby karibu,nimekumisi sana”
Maneno aliyotamka Sonia yalipita vizuri sana juu ya pina za masikio ya Alex Mwandambo yakaingia ndani ya ngoma na kugusa moyo wake,akahisi kama mwili wake umepigwa na baridi na kupata ganzi baada ya kusikia Stuwart kaitwa kimahaba kama hivyo,bila aibu yoyote ile na kwa mbwembwe zote Sonia akamfuata Stuwart midomoni na kufungua kinywa chake,akamshika vizuri Stuwart mdomoni na kuanza kumnyonya lips,wakaanza kulana denda.
“Karibu nyumbani Mme wangu,leo nina mambo matamu nataka kukupa.Lakini kuna mgeni wako hapa”
Jicho alilompiga nalo Alex lilikuwa kiboko,ukiunganisha na macho yake makubwa ndiyo kabisa.
“Bro Alex mbona umeishia nje?karibu ndani ulikuwa hapa muda mrefu?”
Stuwart ndiye alikuwa anauliza swali hilo hakuelewa ni kiasi gani anamchoma moyo Alex licha ya yote hakuelewa lolote ingawa alielewa kuwa Alex alishawahi kuwa na mahusiano na Sonia ndiyo maana akauliza swali ambalo lililochanganyika na chembechembe ya dharau.
“Stuwart”
“Yes broo”
“Unamjua huyu binti sawasawa?”
“Ndiyo ni mke wangu”
“Tangu lini?”
“Muda mrefu,kwani vipi?”
“Wewe Malaya”
Lilikuwa ni tusi kutoka kwa Alex likimlenga Sonia.
“Ningekuwa Malaya ningekuwa najiuza barabarani na isitoshe ningekukubalia hata wewe,Alex naomba utuache nilishakwambiaga sikutaki”
“Rudia tena Hafuan”
“Kitu kingine nisamehe,jina langu sio Hafuan naitwa Rashidah”
“Shit!”
Akex alikema na kushusha pumzi nzito ya kuchoka.
“Broo huyu ni shemeji yako lakini samahani kama alishawahi kuwa mpenzi wako,haina sababu ya kuweke….”
“Nyamaza Stuwart,hujui unachokiongea.Kaa kimnya”
“Punguza hasira broo”
“Nimekwambia kaa kimnya Stuwart,siongei nawewe”
Stuwart akakatishwa hapohapo.
“Kwahiyo umeamua kunidangan…”
“Alex nisikilize nikwambie,siwezi kuwa nawewe sikutaki naomba nielewe sijisikii kuongea nawewe full stop”
Sonia ghafla akajifanya kuwa mkali ili kumkatisha Alex kuongea, hakutaka kumpa nafasi ya kuzungumza ili kuonesha swala lake lina msisitizo alijitoa mikononi mwa Stuwart na kuingia ndani akiwaacha Alex na Stuwart wanatizamana kama mabeberu ya mbuzi zizini.
“Sikiliza Bro wewe niachie huyu demu mimi nampenda”
“Hata mimi nampenda ndiyo maana nikamuacha mke wangu kwa ajili yake”
“Lakini si ulimsikia mwenyewe”
“Stuwart wewe ni ndugu yangu isitoshe mimi ni kaka yako.Huyu mwanamke nimetoka naye mbali.Sisi sote ni wanaume ujue sitaki tuwekeane chuki”
“Naelewa lakini wewe mw….”
Sonia aliyetokeza tena mlangoni ndiye aliyewakatisha.
“Baby njoo ndani tafadhali”
Hapo ndipo Stuwart alipogeuka na kumpa kisogo Alex aliyekuwa nje,hakutaka kugeuka nyuma akaingia na kufunga mlango kwa ndani.

Siku zote majuto ni mjukuu na Alex alikuwa akijilaumu kwa kitu alichokifanya cha kumfukuza mama watoto wake kisha mwanamke huyo ambaye leo hii kamfumania na ndugu yake kumtenda,sura ya mke wake ilijirudia huku roho ikimuuma kupindukia.Alimlaumu Shetani aliyekuwa kuzimu, hakuelewa ni kwa namna gani aende kwa wakwe zake aliowatukana na kuwaomba radhi kwa dharau alizowaonesha,hicho ndicho kitu kilichokuwa kinakula ubongo wake akiwa ndani ya taxi anarejea nyumbani kwake Afrikasana.
***
Kama kila kitu alipewa mapenzi na Mahitaji yote lakini hakuridhika akawa kama ndege mara kiota hiki mara kile,baada ya kuvurugana na Alex na kuamini kuwa tayari keshampa Ukimwi sasa aliamia kwa mdogo mtu Stuwart,hayo ndiyo yalikuwa mahesabu yake ya kuusambaza ukimwi kwenye ukoo unaoitwa Mwandambo.Wakati akiwa na Stuwart mara nyingi alipokea meseji za msamaha kutoka kwa Alex lakini hakuzijibu na wala simu zake hakupokea tena.
Yote hayo aliyafanya Stuwart akiwa anajua.
“Alex bado ananiomba msamaha love”
Sonia alimwambia Stuwart siku hiyo wakiwa ndani ya gari wametoka kuangalia sinema mpya My fair plazza.
“Wewe unamjibu nini?”
“Sijamjibu,mimi nakupenda wewe”
“Kweli?”
“Ndio baby wangu,naomba usije kunitenda”
“Hilo ondoa shaka siwezi kufanya hivyo”
Kwa jinsi alivyokuwa kafanya ngono na Stuwart alijua tayari keshampaka Ukimwi na alichokuwa anasubiri kingine ni kuuteka moyo wake ndiyo maana akajifanya anampemda sana na wakati mwingine alilala naye nyumbani kwake Kijitonyama,maisha yalikuwa matamu kwa wawili hawa na Stuwart alijihesabia yeye ni mwanaume wa shoka, alitembea kifua mbele na kujigamba kupata mwanamke mzuri kama Sonia, hakuelewa kuwa anajipalia makaa ya mawe mwenyewe na mwisho wa siku angekufa kwa kifo kibaya sana cha ugonjwa wa Ukimwi,Sonia aliyafanya haya yote kwa sababu ya kulipiza kisasi ingawa wakati mwingine alijiona mkosaji kuuwa watu wasiokuwa na hatia,aliamini siku yoyote akitoweka duniani basi moto wa shetani jehanam ungemuhusu.
“MBONA HUKUNITAFUTA TENA SASA?”
Ilikuwa ni meseji kutoka kwa Mr.Stanley Mwandambo baba mzazi wa Stuwart,tena alikuwa akichat wakiwa seblen,Stuwart yupo pembeni yake.
“NILISAFIRI KIDOGO,SASA HIVI NIMERUDI”
“UMERUDI?”
Mzee Stanley alituma meseji na kuusindikiza na emoji iliyotoa macho kumaanisha kuwa ameshtuka.
“NDIO”
“UPO WAPI?”
“HOME”
“NAWEZA KUKUPIGIA SM?”
“HAPANA,SASA HIVI NATAKA KULALA NIMECHOKA SANA”
“KESHO UNA RATIBA GANI KWANI?”
“NITAENDA KUTAFUTA KAZI TENA BANDARINI”
“NILIKWAMBIA UJE OFISINI KWANGU,UJE AISEE USIACHE”
“SAWA NITAJITAHIDI”
“UJE TAFADHALI”
“OK”
Hapo ndipo wakaacha kuchat na Sonia,akatupa simu pembeni na kubwaga macho yake juu ya televisheni.
“TANZANIA YAZIDI KUINGIA KIDEDEA NA TIMU YA TAIFA INATEGEMEA KUCHEZA MECHI NA AFGHANSTAN HUKO UWARABUNI,MCHEZAJI ANAYEPEPERUSHA BENDERA YA TANZANIA PARTSON NGOGO AMEZIDI KUNG’AA KWA KUSHINDA MAGOLI MENGI NA MAKOCHA MBALIMBALI WANAMUHITAJI”
Sonia aliitizama televisheni akahisi kichefuchefu cha kutapika,alimchukia sana mwanaume huyo mcheza mpira kwa mambo aliyomfanyia ya usaliti.
“Baby inabidi tusafiri,nataka twende wote tukashuhudie hiyo mechi namkubali sana Partson Ngogo”
Lilikuwa ni ombi kutoka kwa Stuwart.


 Afya ya Brenda ilizidi kukongoroka kila kukicha,alipungua uzito mara tatu yake tofauti na jinsi alivyokuwa mara ya kwanza,kifua na homa kali vilishambulia mwili wake dawa za kifua alishatumia lakini hali ilikuwa vilevile, Mama yake alishaelewa nini maana yake sababu dalili za ugonjwa wa Ukimwi karibia zote alikuwa nazo,shingo ya Brenda ilikakamaa na kuonesha vishimo.Mara kwa mara alikuwa akitapika.
“Mama ko..ho ko…ho”
Siku hiyo usiku alimuita Mama yake huku akikohoa mfululizo.
“Abe..e mwanangu”
Pendo Jonas akaitikia kwa sauti ya kukata tamaa.
“Mbona siponi kifua?kinanisumbua sana,nikikohoa nahisi kinawaka moto”
“Utapona mwanangu usijali”
Ingawa alijua tayari ugonjwa unaomsumbua mwanaye wa pekee Brenda lakini hakutaka kumvunja moyo.
“Siwezi,ninajua nina ukimwi na nimejitakia mwenyewe laiti ningekusikiliza Mama wenda nisingekuwa hivi”
Brenda aliamua kupasua jipu mwenyewe,maneno aliyokuwa akikanywa na mama yake miaka mingi iliyopita sasa yalimrudia na kujuta,Sebastian ndiye aliyemuambukiza ukimwi hilo alilijua naye aliutoa kwa Sonia,damu yake ilikuwa dhaifu na ndiyo maana ugonjwa huo ulimshambulia kwa kasi na kumfanya akonde.
Pendo Jonas alihisi mashavu yake yanalowana na maji,alikuwa akilia bila kutegemea akamuinua binti yake karibu na kumkumbatia.
“Sio kosa lako mwanangu,yote yanayotokea ni mipango tu ya Mungu”
“Hapana Mama usimshirikishe Mungu kwenye jambo hili,naomba unisamehe mimi hata nikifa siku yoyote ile naomba uniombee msamaha kwa dada Sonia”
“Mwanangu usiseme hivyo”
“Naelewa mwisho wa siku lazima tufe lakini huu ugonjwa unaua vibaya sana”
“Brenda”
“Abee Mama”
“Nitafanya jitihada zote ku…”
“Mama usijali acha tu ninastaili tu kufa,nilikuwa mtumwa wa ngono wa Sebastian,sikuelewa lolote nilikuwa mlevi wa penzi lake.Naomba unisamehe kwa kila kitu”
Brenda alikuwa akiongea huku akimwaga machozi ingawa hakuwa na uhakika juu ya ugonjwa unaomtesa kutoka kwa daktari lakini alielewa kila kitu,swala la yeye kuwa na ukimwi lilikuwa wazi kabisa tena kwa asilimia zote mia moja, ndiyo maana alilia kwa uchungu.
“Naom..ba ku..ongea na da..da Sonia tafadhali”
“Sasa hivi?”
“Ndio Mama”
Ingawa ulikuwa ni usiku Mama yake alitafuta simu wakati huohuo,akatafuta namba za Sonia hewani lakini simu iliita bila kupokelewa,akajaribu tena lakini hali ilikuwa hivyo hivyo,simu haikupokelewa Brenda alikuwa akilia machozi muda wote alivyotafakari aina ya kifo alichokuwa anaenda kukikabili, alikiogopa mwenyewe.
Kifo cha ugonjwa huo wa Ukimwi kilianza kumsumbua kabla hata ya kuanza kumshambulia,maumivu aliyokuwa anayasikia akiwa anakohoa yalikuwa makali mno.
“Mwanangu bado sijampata”
“Na…omba kabl..a sijafa niwe nimeonana na Dada So..nia”
Kauli hiyo ilimfanya Pendo Jonas aangue kilio mpaka mume wake aliyekuwa chumbani akatoka mbiombio mpaka chumbani kwa Brenda ambapo aliwakuta wamekumbatiana wanalia machozi.
“Vipi?kuna nini?”
“Hakuna ki..tu mume Wangu”
Pendo hakutaka kuweka mambo wazi.
“Tell him th..e tru..th”(Mwambie ukweli)
Brenda akasema, hapo ndipo Pendo akaanika kila kitu wazi kutoka ndani ya kifua chake,alianza kumuhadithia mume wake kuanzia Brenda alipoupata ugonjwa huo na wapi alipoutoa.Santiago alihisi huruma ajabu,akamtizama Brenda kwa macho yaliyojaa huruma.
“Pole sana,hapa Marekani ugonjwa huo ni wa kawaida sana”
“Kwanini unasema hivyo?”
“Dawa zipo japokuwa ni gharama lakini mimi nitafanya chochote kile ili Brenda azidi kuishi”
Hivyo ndivyo Santiago alivyotoa ushauri lakini kwa Brenda hakuonesha hali yoyote ya furaha aliendelea kulia machozi ya uchungu.

Siku inayofuata Mzee Santiago na Mke wake pamoja na Brenda walisafiri mpaka jiji la Miami katika hospitali iliyoitwa St.Theresa ili kupata matibabu ya Brenda,hospitali hiyo ilikuwa kubwa mno na watu walipata huduma ya uhakika ndiyo maana Mzee huyu Santiago aliamua kuwasha gari lake mpaka nje ya Mji akitokea Los Angeles.
Ni kweli walifika lakini majibu waliyopata yalizidi kuwafanya wakate tamaa.
“Mmechelewa kufika hospitali,wadudu wa virusi walikula sana chembechembe zake za damu na isitoshe grup lake la damu ni dhaifu ndiyo maana kinga zake zilikufa mapema lakini sio mbaya kuna dawa tutampatia wenda muujiza wa Mungu utatokea”
Daktari alikuwa akiongea maneno hayo,Pendo alikuwa akibubujikwa na machozi akasimama na kuegemea ukutani,alilia na kusaga meno mpaka akatoa kamasi hakuwa tayari kuambiwa kuwa mwanaye ana siku chache za kuishi duniani mbali na hapo ugonjwa uliokwenda kumuuwa usingempa heshima yoyote ile mwanaye.
“Bre…nd….a mwanaguuu”
Pendo Jonas alilia machozi Mume wake Santiago akamfuata kwa nyuma na kumkumbatia akijaribu kumfariji lakini haikuwa rahisi hata kidogo.
Waliondoka na Brenda kutoka Miami na kurudi jijini Los Angeles wakiwa wamechoka kabisa,walimuonea huruma sana mtoto wao ambaye muda wote alikuwa akikohoa na alilalamika kuwa anaumia kifua.
Brenda alianza dozi siku inayofuata lakini baada ya mwezi mmoja hali yake ilikuwa mbaya zaidi,alianza kuharisha mfululizo akazidi kupungua uzito kabisa,mashavu yake yakaingia ndani akawa amekonda mno.
Mdomoni akawa ana vitu kama utando wa buibui,mwili wake aliuhisi una waka moto,alitamani siku zirudi nyuma aweke mambo sawa lakini alikuwa amechelewa tayari, ugonjwa aliuopata na kuuchukulia poa ulikuwa ukimtesa kitandani.Akatamani angalau asimame juu angani autangazie ulimwengu kuwa ugonjwa wa Ukimwi ni hatari sana na unatesa kupita kiasi hivyo wasichana wenzake wawe makini lakini ikashindikana kabisa sababu hakuwa na nguvu hata kidogo,chakula hakula tena na hapo ndipo akaanza kutumia mirija ili chakula kipite,alijisaidia akiwa kitandani hapohapo.
“Ma…ma. Naom.ba kuonana na Dada Soni…a”
Brenda alijikaza siku hiyo, aliamini kuwa ana siku chache za kuishi duniani,alitaka kuonana na Sonia walau amuombe msamaha.Kitu kilichomchanganya akili ni kuhusu Sebastian, tangu aanze kuugua hakumtia machoni tena,hilo ndilo likamuumiza zaidi.
****
“Halloo,naongea na nani?”
Sonia alikuwa simuni akiwa kitandani tena juu ya kitambi cha Mzee Stanley Mwandambo baba mzazi wa Stuwart baada ya kutoka kufanya naye ngono zembe bila ya kutumia zana yaani nyama kwa nyama,alihakikisha mzee huyo hatoki na ni lazima ampake maradhi ya Ukimwi na ukoo mzima upate ugonjwa huo wa Ukimwi,alijiona yupo sahihi ingawa alijua hilo halikuwa suluisho na ndiyo maana aliendelea kuusambaza Ukimwi,mama yake alifia kitandani kwa maradhi hayohayo nayeye alifanya hivyo hivyo ili kukomoa ndiyo maana hakujuta,alijisikia amani sana.
Laiti wanaume wangejua anachofanya Sonia wangempiga risasi wamuuwe,hakuna mtu aliyekuwa yupo tayari kuupata ugonjwa huo hatari wa ukimwi na kwa jinsi Sonia alivyonawiri isingekuwa rahisi kwa mtu yoyote yule kumgundua.
“Unaongea na Pendo,Mama yako”
Sonia alikaa sawa kitako na kumuacha Mzee Stanley Mwanadambo akiwa chali anamtizama haamini kama ndiye yeye yupo na mwanamke mzuri kiasi hicho.
“Mama,habari za siku nyingi?Shikamoo”
“Nzuri tu mwanangu.Nikuombe kitu?”
“Bila shaka Mama yangu”
“Unaweza ukasafiri na kuja Marekani?”
“Lini?”
“Ikiwezekana ukipata viza tu,mimi nitakutumia invitation letter ili wasikuzungushe”
“Kuna tatizo lolote?”
“Hapana mwanangu wewe njoo”
“Hakuna shaka,nitumie invitation mimi nitakuja,Brenda mzima?”
“Brendaa,yeye mzima”
Pendo alificha lakini Sonia alianza kuchezwa na machale kuwa kitu anachoitiwa hakikuwa cha kawaida na alihisi itakuwa lazima ni kuhusu Brenda.
“Sawa Mama usijali”
Mawasiliano yakaishia hapo yakimuacha Sonia akiwa katika mawazo tele.
“Vipi mpenzi wangu?”
Mr.Stanley Mwandambo alimuuliza Sonia baada ya kumuona kabadilika ghafla.
“Hakuna kitu,usijali”
“Njoo basi hapa”
“Hapana,ngoja nirudi nyumbani”
“Bado nina hamu mwenzio”
“Nitakuja Usiku,tukutane”
“Kweli?”
“Ndio baby”
***
Alex Mwandambo alihisi kujuta sana na alichotakiwa kufanya ni kuomba msamaha kwa mke wake ili warudiane walee watoto,alimuonea huruma mke wake Latifah,aliamini kuwa anastaili adhabu ama laana kubwa.Alimlaumu sana ibirisi kwa kitendo alichokifanya cha kuitenganisha familia yake.
“Lazima nikamuombe msamaha Latifah”
Siku hiyo asubuhi alivyojiandaa na kuvaa koti la Suti alighaili kwenda kazini badala yake safari ilibadilika na kufikiria kufika Bagamoyo ili akaonane na Latifah waweke tofauti zao kando wawe kama zamani na waitunze familia.
Alitembea mpaka nje kwenye maegesho ya magari,alivyopita seblen alihisi kuna kitu kilikosekana,mabusu ya mke wake kila asubuhi akimuaga kwenda kazini na kumtakia kazi njema.Hapo ndipo aliamini kuwa Shetani yupo na aliulaumu mwili wake, tamaa zake za mwili na hisia zake kwa Sonia zilimponza.

Alivyofika nje alitembea mpaka kwenye gari lake aina ya Prado akafungua mlango na kuingia ndani,alilirudisha kinyume nyume na kuweka gia namba moja tayari kwa kutoka nje ya geti,Mlinzi akafungua geti akatoa gari nje.
Akiwa ndani ya gari nyuma ya Usukani alitingwa na mawazo chungumzima,kusamehewa kwake kulikuwa hamsini chini ya mia moja,yaani nusu kwa nusu.Na jambo hilo alilifananisha kama mchezo wa kamali kupuna ama kukosa,ndiyo maana alijaribu bahati yake.
Alichokifikiria yeye ni jinsi gani angeweka uso wake kwa Baba yake Mkwe aliyemfukuza nyumbani kwake kama Mbwa hilo ndilo likamuogopesha zaidi.

Baada ya lisaa limoja na dakika arobaini alikuwa anaipita Bunju na kuendelea kunyoosha mguu,alishusha gia na kukunja kona ambapo alisimama pembeni ya maduka ya jumla ya vyakula.Muuza duka alivyoliona gari akalikimbilia harakaharaka.
“Shikamoo Mzee”
Japokuwa muuza duka alikuwa na umri kumzidi Alex lakini alitoa salamu,kwa harakaharaka alikuwa ni mzee wa umri wa miaka sitini lakini alimsalimia Alex kwa adabu zote,maisha magumu ndiyo yalimfanya awaamkie hata aliowazidi umri.
“Nipatie magunia mawili ya mchele,una sukari?”
Alex aliipotezea salamu na kushuka ndani ya gari.
“Sukari ipo, unga pia upo kila kitu kipo”
Mzee aliongea na kumuonesha mteja wake kile anachohitaji,Alex alinunua magunia matatu ya mchele,mawili ya sukari na moja la unga.Hakusahau mafuta ya kula dumu moja pia.Akamlipa Mzee muuza duka na vikapakiwa ndani ya gari.
Akaingia ndani ya gari hapohapo safari ikaanza,Alex hakutaka kwenda kuomba msamaha akiwa mikono mitupu akiamini ile methali inayosema mkono mtupu haulambwi.
Akazidi kunyoosha mguu na alivyofika kwenye kibao kilichoandikwa Migombani Bar,akakunja kushoto na kuchukua barabara ya vumbi,alikuwa tayari amekabiria nyumbani kwa Mke wake Latifah ingawa bado alikuwa amebakisha umbali wa kama mita mia moja na ushehe!
Moyo wake ulizidi kumdunda kwa nguvu alivyoona minazi miwili na nje kulikuwa na nyumba ya matofali yenye kibaraza kilichochakaa,watoto wanacheza mdako,hapohapo aliweka gari kando na kusimama,akashuka ndani ya gari.
“Daaaaaad”
Mackline mtoto wake wa kwanza wa kike ndiye alimuona Baba yake na kumrukia,Alex alihisi uchungu ajabu.
“Umefuata nini kwetu?Mackline ingia ndani”
Latifah ndiye aliyetokeza mlangoni na kuongea kwa hasira.
“Nimekufuata wewe Latifah”
“Tafadhali naomba uwende,unadhani ukiniacha ndiyo nitakufa maskini.Sawa kwetu sisi ni maskini laki..”
“Latifah tafadhali naomba tuongee”
“Siwezi kuongea nawewe,Mackline ingia ndani”
Latifah akamvuta mwanaye wakaingia ndani na kumuacha Alex nje analengwa na machozi hajui ni kitu gani akifanye.
“Latifah,fungua mlango tuongee mke wangu….Latifah”
Alex alibakia Mlangoni akiita lakini hakuitikiwa ingawa hakuruhusiwa kuingia ndani lakini alikaa chini na hakutaka kurudi kama alivyotoka ilikuwa ni lazima arudi na mke wake nyumbani ndiyo maana akaweka makalio yake kibarazi hakutaka kubanduka.
Kilichomuogopesha zaidi na kilichomfanya asimame kwa adabu ni baada ya kumuona Baba Latifah ameweka jembe begani ametokea shambani kulima.
“Shikamoo Baba”
Alex alisalimia,lakini Mkwewe kabla ya kumuitikia alimuangalia kwa kitambo kidogo.
“Marahaba”
Alivyomjibu akagonga mlango,Latifah akatoka akiwa analia machozi macho yake yakagongana na Alex,kuna kitu kilikuwepo moyoni mwa Latifah si kingine bali ni Mapenzi ya dhati.
Alihisi kumsamehe Alex lakini upande mwingine wa moyo wake ulisita.
“Latifah”
“Ah ah abeee”
“Naomba unisamehe”
Katika maisha yake Alex hakuwahi kupiga magoti hiyo ndiyo ilikuwa siku yake ya kwanza kumaanisha kuwa jambo analotaka alilimaanisha.
Samehe saba mara sabini na hivyo ndivyo alivyoamini siku zote Latifah na katika maisha yake alifundishwa kitu kusamehe alivyokuwa anasoma Masjid,akamuinua Alex na kumkumbatia.
“Nime...kuku..samehe Mume wa...ngu”
Aliongea huku akilia kwa uchungu.
“Ahsante mke wangu”
“Lakini kwa sharti moja”
“Niambie tu,ili mradi utanisamehe”
“Tukapime kwanza afya zetu”

 Kwa Alex halikuwa tatizo kwake ndiyo maana hakuwa na wasiwasi wowote ule kuhusu afya yake, wakaingia ndani ya gari na safari ya kwenda zahanati ya karibu kuanza mara moja.Moyo wa Alex ulikuwa mweupe kabisa,wa kwanza akawa yeye kuingia ndani ya chumba cha kupimia virusi vya Ukimwi tena akiwa mwenye tabasamu pana.
“Dokta kwema?”
Alex alimsabahi daktari.
“Karibuni sana”
“Ahsante tunashukuru”
“Mimi mwenzenu naitwa Dokta Nelson Matimba,sijui wenzangu”
“Mimi naitwa Alex Mwandambo huyu ni Mke wangu anaitwa Latifah,tumekuja kupima afya zetu”
Baada ya utambulisho mdogo dokta Nelson alianza kuwahoji maswali ya hapa na pale ili kuwatoa wasiwasi, wote walitulia ili kumsikiliza kile anachokiongea na hakuna hata mmoja aliyeonesha wasiwasi wowote ingawa moyo wa Latifah ndiyo ulikuwa unakita kupita kiasi japokuwa hakuwahi kuwa na mwanamme mwingine zaidi ya Alex,jambo alililomshauri mume wake alifanye aliliogopa mwenyewe.
“Alex”
Latifah akaita kwa upole.
“Naam”
“Wewe hauna wasiwasi?”
“Hapana,kwanini niwe nao ninajiamini”
“Mimi moyo wangu unadunda,sijui kwanini”
“Punguza Presha”
Alex na Latifah waliteta baada ya dokta Nelson kuingia maabara ili kuziangalia damu zao.
“Mme wangu nikuulize swali?”
“Uliza tu”
“Mfano majibu yakitoka mimi nina Ukimwi utaendelea kuishi namimi?”
Lilikuwa ni swali lililomfanya Alex amuangalie Mkewe kwa kitambo kidogo bila kutoa jibu la harakaharaka, lilikuwa ni swali la mtego ingawa lilihitaji jibu hapohapo.
“Kwa kweli Latifah hilo ni swali gumu,tuombe Mungu usiwe nao maana…”
“Maana nini?”
“Naomba tusubiri majibu”
Kupitia macho ya mume wake kuna kitu aliweza kukisoma kwamba endapo majibu yangetoka na kuonesha ana maambukizi ya Ukimwi basi huo ndiyo ungekuwa mwisho wao kuishi wote kama wanandoa,Latifah aliwaza sana na kuanza kujutia maamuzi aliyochukuwa na kutaka kwenda kupima Ukimwi siku hiyo,sababu hakujiamini, akiwa kimnya amejikita kwenye dimbwi la mawazo Dokta Nelson akatokeza na hapo ndipo mapigo ya Latifah yakaongeza kasi ya kudunda,alianza kuogopa kabla hata majibu hayatolewa.
“Majibu yenu yapo hapa”
Dokta alisema na kuvua miwani akaweka juu ya meza kisha kuwatazama wanandoa hawa waliofika kujua afya zao.Alivyogonganisha macho yake na Latifah aligundua ni jinsi gani alivyokuwa mwenye wasiwasi kupita hata Alex.
“Dokta,majibu yanasemaje?”
Alex alitaka kujua hakutaka kupotezewa muda na aliuliza kwa kujiamini.
“Mr and Mrs Alex Mwandambo nadhani mpo tayari kwa majibu yoyote yale?”
“Ndio”
Wote wakaitika kwa pamoja.
“Kuna mmoja kati yenu ana virusi vya Ukimwi lakini hiyo haimaanishi ndiyo mwisho wenu mtaendelea kuishi kama kawaida na mtaendelea kushiriki tendo la ndoa endapo mtafata utaratibu”
Moyo wa Latifah ukapiga paa!Alex akamkata jicho kali la chuki na katika akili yake ilimtuma moja kwa moja kuwa Latifah ndiye ana Ukimwi,hapohapo alimgeukia daktari.
“Dokta embu toa majibu yaliyonyooka nani ana Ukimwi?”
“Naomba upunguze Jazba Mr.Alex”
“Niambie tu kama ni mke wangu mimi sitomuacha,nitaendelea kumpenda nachotaka ni kupata tu uhakika”
“Mkeo yupo salama,hana maambukizi ya ukimwi damu yake ipo safi”
Waliokuwa wameenda kupima damu zao ni wawili,Alex na Mkewe.Majibu ya dokta ingawa yalieleweka lakini hakutaka kuyanyoosha moja kwa moja,alizunguka mbuyu kidogo.
“Dokta bado sijakuelewa”
Latifah akauliza kwa upole.
“Majibu yako yako safi,damu yako haina maambukizi ya ukimwi”
“Ukiwa una maana gani?”
“Mume wako ndiye ameathirika”
Ndani ya uti wa mgongo wa Alex alihisi kama amepigwa na baridi,masikio yake hayakuwa tayari kukubaliana na ukweli kwamba ugonjwa wa ukimwi anao mwilini mwake jambo ambalo hakulitegemea kabisa katika maisha yake,aliamini ukimwi upo duniani lakini hata siku moja hakuwahi hata kuota kama ungempata mtu kama yeye,hiyo ndiyo ikamvuruga akili yake mazima!
“Dokta…Acha masihara sasa”
Majibu ya dokta bado aliendelea kuyatafakari kichwani kuwa sio ya ukweli ni ya kugushi.
“Latifah tuondoke naona huyu daktari sasa ana..”
“Alex”
“Haya majibu sio ya ukweli twende kwingine kwanza hapa kijijini hakuna huduma nzuri vipimo vyao vya kishamba, mimi nitakuja kumshtaki huyu dokta bwegenazi huyu”
Alex alibisha mwanzo mwisho na kutoa maneno ya kashfa,akamuinua mke wake na kutoka nje,ambapo huko waliingia ndani ya gari na safari ya kwenda mjini kuanza.

Ndani ya gari Alex aliendelea kumlaani Dokta Nelson kwa kutaka kujaribu kutoa majibu ya uwongo,walivyofika Tegeta kwa ndevu katika Hospitali ya Dokta Kimaro wakasimama na kushuka.
“Labda hapa kwa rafiki yangu Kimaro ndiyo nitapata majibu ya uhakika,embu tushuke”
Wote walishuka tena na kupanda ngazi na bahati nzuri Alex alikutana na rafiki yake Dokta Kimaro ambaye walisoma wote nchini Uingereza nayeye akaamuma kurejea Tanzania kufungua hospitali binafsi baada ya kufanya kazi muda mrefu katika Hospitali ya taifa ya Muhimbili.
“Alex”
“Dokta Kimaro”
“Za siku nyingi kiongozi”
“Aise salama,za majukumu?”
“Safi tu,mimi ndio nimefika bwana”
“Sawa njoeni ofisini kwangu”
Hata kabla ya kukaa Alex na Mke wake wakanyoosha mpaka ndani ya ofisi ya Dokta kisha kuketi.
“Shemeji za siku nyingi?”
Dokta Kimaro alimsabahi mke wa Alex.
“Salama shemeji”
“Mara ya mwisho kukuona ilikuwa Mwaka jana kwenye sendoff ya Prisca Mwakyembe,hivi Alex hakuwepo eeh?”
“Alikuwa South Africa”
“Yah Kweli,enhee vipi Bwana mkubwa.Naona leo umenivamia”
Dokta Kimaro akaweka utani kidogo kwa rafiki yake na wote wakatabasamu.
“Ndio,sijui kwanini madaktari wa hapa bongo wanakuwa feki.Mimi ndiyo maana nasema kuwa hapa bongo bado sana”
“Kwanini unasema hivyo?”
“Nilienda Hospitali moja hivi ipo huko vichochoroni,hospitali ochwala waswaili wanasema.Eti wanadai nina ukimwi.Hilo linawezekana kweli?”
“Enhee sasa ikawaje?”
“Ndio nimekuja hapa kwako Kimaro,mwenyewe unipime unipe majibu ya Ukweli”
“Kwahiyo umekuja kupima,au mmekuja kupima?”
“Tupime tu wote”
Dokta Kimaro bila kupoteza wakati akachukuwa damu zao kubwa na kuingia nazo maabara,dakika kumi zilikuwa nyingi akawa amefika ofisini kwake na karatasi mbili mkononi,sura aliyoingia nayo haikuwa ya kawaida,alimtizama Alex kwa macho yaliyojaa huruma.
“Vipi Kimaro?”
Alex aliuliza kwa kihoro,lakini Dokta hakujibu kitu aliinamisha kichwa chake, hakuelewa ni kwa namna gani ayatoe majibu aliyokuwa nayo.
“Dokta Kimaro,nipe majibu”
“Alex”
“Naam ndugu”
“Majibu yalikuwa sahihi,damu yako ina virusi vya Ukimwi”
Hayo ndiyo yalikuwa majibu yake hata angesafiri na kwenda nje ya nchi kupima damu ukweli ungebaki palepale kwamba ameathirika na Ukimwi.Latifah alikaa kimnya ingawa ugonjwa huo hakuwa nao lakini hata yeye aliogopa mno,mwili wake ulimtetemeka sababu alijuwa nini mwisho wa ugonjwa huo.
****
Ugonjwa hatari wa Ukimwi ulizidi kusambaa kwa kasi ya umeme nchini Kenya sababu Leythan alikaribia kumaliza wanawake wote waliokuwa Mombasa na wengi wa Wasichana au Wanawake aliotembea nao walikuwa wake za watu,walipeleka gonjwa hilo kwa wame zao pia waume zao waliusambaza kwa michepuko, mnyororo ukawa mrefu,takwimu ilivyotoka August 2001 ilionesha kuwa asilimia sabini na moja wana maambukizi ya Ukimwi.
“Unasemaje baby?”
“Njoo mara moja”
“Wapi?”
“Hapa nje”
Japokuwa Leythan alitemwa na Conie lakini aliendelea kudunda ingawa afya yake ilikuwa dhaifu kimtindo!
“Baby,mbona umepungua hivyo?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa demu wake mpya aliyeitwa Sakina.
“Ah hata sijui”
“Au hauli mpenzi wangu?”
“Nakula,nakuwaza wewe ndiyo maana”
“Ndio upungue hivyo?”
Ni kweli ungebahatika kumuona Leythan alivyo na jinsi alivyokuwa awali ungeungana na maneno anayosema Sakina kwamba amepungua mno na kilichomfanya apungue alidhani wenda ni mawazo tu ya kawaida hakuelewa kuwa tayari ana ugonjwa wa Ukimwi.

Wakati wanazungumza mambo yao ndani ya Magahawa kona ya kushoto alikuwa ameketi Afande Maria na askari mwenzake na tayari walishahakikisha kuwa Leythan wanayemtafuta ndiye yeye.
“Kwahiyo tunaenda kumkamata?”
“Ndiyo,unaogopa?”
“Conie yupo wapi?”
“Nilimpeleka Kituo kikubwa kule Mjini”
“Sawa,wacha niende mimi”
Afande Maria akasimama wima na kutembea mpaka kandokando ya meza aliyokaa Leythan na Mpenzi wake Sakina ambaye alikuwa anamuweka mjini.
“Habari hapa,sina mazungumzo mengi sana.Leythan kuanzia ninavyoongea nawewe sasa hivi upo chini ya ulinzi”
“Wewe demu vipi?”
Leythan alikema na kutaka kusimama lakini alitulizwa na ukofi kutoka kwa Afande Maria.
“Tulia,usijaribu kufanya zoezi hili likawa gumu”
Hapohapo Afande Maria akatoa kitambulisho na kumuonesha Leythan.
“Nadhani unajua ulichokifanya Dar es salaam wewe na Conie”
“Sio mimi jamani”
Leythan alisimamishwa juu juu,wakaongozana na Maria mpaka kwa askari mwenzake.Hawakutaka kupoteza wakati wakaingia ndani taxi na safari ya kwenda kituo kikubwa cha Polisi alichohifandiwa Conie kuanza mara moja!
****
“Mume wangu usijali,bado nitaendelea kukupenda hata kama unaumwa.Huo ni ugonjwa kama mwingine”
“Hapana Latifah,sitaki kukuuwa”
“Usijali Alex mwisho wa siku kila binadamu ataonja umauti,wewe ni mume wangu tatizo lako ni tatizo langu pia”
“Sawa nimekuelewa Mke wangu”
Jinsi alivyojibu Alex kwa kukata tamaa kulimfanya mkewe aingiwe na wasiwasi mno.
Alex alijionea huruma mwenyewe na alishindwa kuelewa ugonjwa huo wa ukimwi ni wapi alipoutoa,aliwaza wanawake aliotembea nao lakini wasiwasi wake mkubwa ulikuwa kwa Sonia au Hafuan kama alivyozoea kumuita.Siku hiyo ilikuwa ni asubuhi baada ya kutoka kuongea na mke wake.
“Usijali kama dokta alivyotueleza tutakuwa tunatumia kondomu”
“Naomba unisamahe mke wangu hata wanangu Mackline na Jamal wakikuwa utaniombea msamaha kwao,uwaambie ukweli”
“Usiseme hivyo”
Alex alihisi kukata tamaa ya kuishi,alikuwa mpole na ndiyo maana aliongea huku akisikitika mno.Alivaa nguo yake vizuri kwa ajili ya kwenda kazini,kichwa chake hakikuwa sawasawa siku hiyo.
“Kazi njema mme wangu”
Latifah alisema akamfuata mme wake mdomoni na kumpiga busu kisha kumuweka tai yake vizuri kooni.
“Ahsante nawewe ubaki salama”
Alex aliwaza kufa,kila alipofikiria aina ya kifo anachokwenda kukabiliana nacho hakupata picha sawasawa, ugonjwa wa ukimwi ni kweli aliuogopa licha ya Mke wake kumpa moyo.Aliingia ndani ya gari lake na kuchukuwa simu yake ya mkononi akijaribu kutafuta namba fulani.
“Halloo Baba Mdogo shikamoo,ndio upo wapi?sawa nakuja sasa hivi hapo kwako.No no no no no kila kitu kipo sawa,nahitaji tu kukuona,kila kitu kipo kwenye mstari.Ahsante nakuja hapo kwako Baba mdogo okay shukrani..Kitu kingine..Ndio nahitaji kuzungumza nawewe.Nakuja sasa hivi siendi kazini leo.Sawa baada ya dakika kama thelathini hivi,okay”
Alex alikataka Simu na safari ya kwenda kwa baba yake mdogo Stanley ndiyo jambo lililomjia kichwani kwa wakati huo.

Kwa kuwa haikuwa mbali na hapo kwa hesabu za harakaharaka ilichukuwa kama dakika Arobaini hivi.
Aliendesha gari kwa mkono mmoja huku mwingine ukiwa umeshika tama ,mawazo yake yapo mbali sana.Aliendesha gari mpaka Tegeta Kibaoni na kukunja kushoto ambapo kulikuwa kuna nguzo nyingi za transfoma hapo alinyoosha mpaka nje ya geti kubwa jeusi ndani kulikuwa kuna gorofa kubwa la kifahari,Stanley Mwandambo baba yake mdogo aliyemsomesha ndiye alikuwa akiishi ndani ya jumba hilo la kifahari, akapiga honi mara moja Mlinzi wa getini akasukuma geti akaingiza gari ndani,akazima gari na kushuka.
“Alex”
Sauti iliyotoka juu ndiyo iliyomshtua alikuwa ni baba yake mdogo akiwa gorofani ameshika glasi ya mvinyo asubuhi na mapema.
“Naam shikamoo”
Huku shingo yake ikiwa juu alisamilia.
“Marahaba mwanangu karibu”
“Ahsante”
“Pita ndani”
Alex alitembea mpaka mlangoni na kufungua mlango ambapo alipita mpaka Seblen na hapo alimuona baba yake mdogo anashuka ngazi wakapeana mikono na wote kuketi juu ya masofa.
“Wewe sio mgeni bwana nenda jikoni kajisevie juice”
“Okay ngoja niende”
Alex akasimama na kuelekea jikoni,alivyokunja kona akapigwa na butwaa la waziwazi hakuamini kile alichokiona,wenda alidhani yupo ndotoni mbele yake alisimama Sonia akiwa amevaa shati la Baba yake mdogo na chupi nyeupe,alimtizama mwanamke huyo aliyekuwa na ‘headset’ masikioni hana habari anasikiliza nyimbo,hakuelewa amfanye nini mwanamke huyu ambaye pia alimfuma kwa ndugu yake Stuwart na leo hii yupo ndani ya jumba la baba yake mdogo,MR.STANLEY MWANDAMBO!


 Mapigo ya moyo ya Alex yalimdunda yakasukuma damu yake kwa kasi,mwanamke aliyeivuruga ndoa yake akamgombanisha yeye na ndugu yake pia, leo hii yupo ndani ya nyumba ya baba yake mdogo,haikuwezekana kuamini hata kidogo kwamba ndugu hao wamechanganywa kama karata!
“Wewe Malaya unafanya nini hapa?”
Alex aliuliza baada ya kuchomoa ‘headset’alizokuwa nazo Sonia masikioni mwake hata yeye alivyomuona Alex alishtuka akatamani kukimbia lakini alishindwa nguvu zilimuishia, ingawa hakutaka kuliweka swala hilo usoni mwake.
“Nipo kwa Mume wangu,wewe umefuata nini?”
Hivyo ndivyo alivyojibu Sonia kwa jeuri na kiburi chote kwa dharau,hakutaka kumuangalia Alex akageuka na kushika mwiko ili aendelee na upishi lakini alihisi maumivu makali kichwani baada ya nywele zake kukamatwa, akavutwa kando na Alex aliyeshikwa na jazba.
“Alex niachieeee,unaniumizaa”
Sonia alipiga kelele kwa sauti ya juu makusudi ili ahakikishe inafika seblen na hivyo ndivyo ilivyokuwa.Mzee Stanley Mwandambo akatokeza jikoni kama mtu aliyeambiwa nyumba yake inaungua na moto,kelele za kipenzi chake zilimshtua ndiyo maana akakurupuka.
“Alex vipi?”
Hilo ndilo swali la kwanza kulitupa Stanley baada ya kuona tukio hilo.
“Wewe Alex…”
“Naam mzee,huyu mwanamke ni Malaya”
“Alex si nilikwambia sikutaki mbona hunielewi?naomba uniache na maisha yangu.Sikutaki”
Sonia aliropoka kwa nia ya kuwachonganisha na alikuwa mjanja aliongea vitu hivyo mbele ya Mzee Stanley aliyetaka kujua chanzo.
“Alex,embu njoo hapa”
“Mzee huyu mwanamke am…”
“Nyamaza,nyamaza nimekwambia.Usinifanyie fujo ndani ya nyumba yangu”
“Mzee naomba ni..”
“Nyamaza guluguja wewe!huna adabu toka kwangu.Toka kwangu”
“Mzee laki…”
“Toka nyumbani kwangu,toka nyumbani kwangu sitaki kukuona tena hapa mshezi wewe huna adabu”
Siku zote Mzee Stanley alikuwa ni mkali hata alivyomlea Alex baada ya baba yake kufariki ndiyo maana aliogopa kupita kiasi,kwa kitendo alichofanya Alex ndani ya nyumba yake alikichukulia kama utovu wa nidhamu na hakutaka jambo hilo liendelee.
“Ondoka Alex”
“Nisamehee Mzee wangu”
“Nimekwambia toka nje,askariii askarii wewe Onyango njoo umtoe huyu na sitaki kumuona tena hapa kwangu”
Alex alihisi uchungu ajabu kitendo cha kugombana na baba yake mdogo kisa Sonia ndiyo kilimuuma mno.Aliingia ndani ya gari lake pembeni akisindikizwa na mlinzi wa getini.
“Umenisikia Onyango,sitaki kumuona huyo mtu hapa nyumbani kwangu tena”
“Sawa bosi”
Mlinzi akakikimbia getini na kulifungua,hakukuwa na namna nyingine ya kuomba msamaha kwa baba yake mdogo aliwasha gari na kulitoa nje akiwa na uchungu kifuani,hasira zilimkaba na kitu kilichomuuma zaidi ni kuhusu ugonjwa wake aliokuwa nao mwilini.
“Mungu wangu,Hafuan”
Kuna kitu kilimshtua kichwani mwake kikamtuma kuwa ni lazima Sonia ndiye anasambaza ugonjwa huo wa Ukimwi,aliendesha gari akiwa mwenye mawazo mengi mno.
Ghafla pepo baya la kuuwa likamvaa,aliamini kuwa endapo asipomuuwa Sonia ukimwi utaendelea kusambaa.Alijuwa kwamba kama yeye ana ugonjwa huo basi na ndugu yake Stuwart pia anao hata baba yake mdogo vilevile.
“Lazima nikuuwe Hafuan namimi nijiue”
Alex aliapia na kupandisha gia,hakuelewa ni wapi anaenda lakini alichojua yeye yupo ndani ya gari tena barabarani.
***
“Target is moving west,on my mark”
“Copy that”
Jeshi la Marekani tayari lilikuwa ndani nchini Afghanstan kuwakomboa wamarekani waliokuwa wanachinjwa na Yusuph Bin Laden katika jiji la Kabul nje ya ngome inayolindwa kuliko ya Raisi,walikuwa umbali wa mita kama elfu nane wengine wapo juu ya gorofa na wengine wapo chini.
Ndani ya jengo hilo kabla ya kuingia ilikuwa ni lazima wawe makini kupita kiasi ndiyo maana wakaingia kimnyakimnya wakisaidiwa na mitambo maalum.
“I’m taking him out,i repeat i’m taking him out i have a clear shot”
“Take it”
Mawasiliano ya kijeshi yalikuwa yakiendelea kimnya kimnya wakitumia vitendea kazi maalum ambavyo vilikuwa vinasikika kwa kila mwanajeshi,aliyetakiwa kuuwawa wa kwanza ni mwarabu aliyekuwa juu ya ngome hiyo analinda usalama.
“Pyuuu pyuu”
Hapo hapo akadondoka chini baada ya kutunguliwa na ‘sniper’ kimnya kimnya iliyokuwa na kiwambo na kutoa sauti.
“You are Clear to move”
Amri ikatolewa,Wanajeshi wawili wakaingia ndani ya geti ili kuanza operesheni yao walikuwa na mitutu ambayo imewekwa vifaa maalum vya kuzuia kelele.
***
Kila siku ilikuwa ni lazima wamarekani wawili au watatu wachinjwe shingo zao na video zitumwe Marekani moja kwa moja ikulu kwa Rasi Obama wakimuonesha kwamba watamaliza raia wao wote,wamarekani walitandwa na hofu na watu walipotea kila kukicha, taarifa zilipomfikia Aidan Waytte kuwa mwanaye kapotea hofu ilimtanda kupita kiasi,alivyojaribu kufuatilia akapata fununu kuwa yupo nchini Afghanstan ametekwa nyara,roho ilimuuma kupita kiasi lakini hakuwa na jinsi Mke wake alilia na kusaga meno sababu ndiye alikuwa ni mtoto wake wa pekee,ndege zilizokuwa zinafanya safari zake kwenda nchi za kiarabu zote zilitunguliwa na makombora kama sio kutekwa nyara hali ikazidi kuwa mbaya sana,Wamarekani wakazuiwa kusafiri kutoka nchi yoyote ya kiarabu,Mzee Aidan Waytte kila alipojaribu kuomba ruksa ili asafiri alikataliwa katakata,Raisi Obama alizidisha ulinzi ndani ya nchi yake huku kimnya kimnya akifanya mawasiliano na majeshi yake yaondoke kimnyakimnya.

Wanajeshi walianza safari baada ya siku mbili wakitumia jambizi chini ya maji.Na kila lililokuwa linaendelea lilifika makao makuu ya Jeshi la Marekani.
“Allah Akbar”
Ulikuwa ni usiku wa saa tatu juu ya alama kwenye mitandao ‘online’,alionekana mtu kapigishwa magoti kisu kipo shingoni tayari kwa kuchinjwa,alikuwa ni mmarekani na kama kawaida ya waarabu walijaribu kutuma ujumbe Marekani.
“Oh My God Sebast….”
Aliyekuwa ameshikiwa kisu alikuwa ni mtoto wa tajiri Waytte na Mama alivyoona video hiyo siku hiyo mtandaoni alidondoka chini na kuzirai.
***
Moyo wa Sebastian ulipiga kwa nguvu ukataka kutokeza nje ya kifua,kisu kilikuwa shingoni mwake na dakika mbili baadaye aliamini angeungana na marehemu wote waliotangulia kwa kukatwa shingo yake na waarabu waliokuwa na hasira,aliamini kuwa ni bado mapema kufa tena kwa kuuwawa kwa kuchinjwa kama kuku.
Alikuwa amepigishwa magoti anatizama kamera iliyokuwa mbele yake inamrekodi, pembeni yake kulikuwa kuna mwarabu amejifunika uso wake kashika kisu kirefu usiku huo,alivyogeuka kushoto kwake alimuona Nasra analia machozi ya uchungu na alimuonea huruma sana sababu baada ya yeye kuchinjwa aliamini Nasra angefuatia,alijaribu kuwaza vitu vingi hasa aina ya kifo anachoenda kupambana nacho cha kukatwa kichwa,akakumbuka kuku anavyochezesha miguu yake kabla ya roho yake kutoka,hapo ndipo alipohisi mashavu yake yanalowana, alilia kwa uchungu.

Wakati hayo yanaendelea Jeshi la Marekani lilikuwa nje tayari linazidi kuingia ndani,waarabu kumi na tisa walikuwa chini wameuwawa na jeshi likazidi kusonga mbele,haikuwa kazi ngumu kwao sababu walitumia mitambo ya kisasa na kupitia ‘satelite’ walielewa ni wapi mateka walipowekwa.Wanajeshi walikuwa wengi nje kama kumbikumbi bila ya Waarabu kuelewa lolote na tayari walinzi wote wa nje walikuwa chini wamekufa kwa kupigwa na risasi,jambo lililobaki lilikuwa ni kuingia ndani ya chumba kilichokuwa kina mateka mia moja na mbili,wote wanasubiri kuchinjwa.Hapo ndipo wanajeshi walipoanza kutega mabomu yao ukutani na mlangoni na waliyategesha dakika tano na lingine dakika sita,wote wakarudi nyuma ili kusubiri zifike dakika sifuri mlango upasuliwe na bomu ingawa mahesabu yao yalikuwa ni kuingia pembeni walipotega bomu la dakika sita.
“Tano,nne,tatu,moja,sifuri”
Baada ya dakika hizo kuisha ulisikika mlipuko mkubwa sana mlango ukapasuka,Waarabu wakaacha shughuli ya kuchinja wakageuka na kushika silaha zao wakizielekezea mlangoni.
Hawakukaa hata dakika moja kwa nyuma ukatokea mlipuko mwingine hapo ndipo wamarekani walipoingia kufanya ‘ambush’na kilichosikika zilikuwa ni risasi kwa kwenda mbele.Kutokana na kujipanga kwa jeshi lao, Waarabu walipukutishwa na risasi na kudondoka kama majani ya miti.
“Nasraaaa”
Sebastian ndiye alikuwa akiita baada ya mwarabu mmoja kuwageukia mateka na kutaka kuwamiminia risasi,Sebastian hakuwa na jinsi zaidi ya kumrukia mwarabu huyo.
Wakaanza kushindana nguvu,Sebastian alishindwa nguvu akamiminiwa risasi tatu za tumbo,akadondoka chini akiwa ameshika tumbo lake damu zinamvuja,hapohapo Mwarabu alipigwa nayeye risasi na jeshi baada ya kuonekana.Ndani ya dakika tano kila kitu kilikuwa kimetulia na mateka wote walikuwa huru,Nasra aliumia moyo kupita kiasi Sebastian alikuwa chini utumbo wake ulikuwa nje amekufa tayari kwa kuchanwa na risasi.

Baada ya tukio hilo kuisha taarifa zilipelekwa moja kwa moja makao makuu kuwa kila kitu kipo sawa na kwa kuwa kikosi kilijipanga helikopta tatu kubwa zilitua nje ya ngome hiyo wamarekani wote wakaingia ndani ya Helkopta,zikazungusha mapanga boi zikapaa hewani.
Aidan Waytte na mke wake walipokea habari za msiba kwa masikitiko makubwa sana mtoto wao Sebastian aliuwawa akijaribu kuwaokoa wenzake na jina lake lilitangazwa katika kila chombo cha habari.Muda wote Nasra alilia machozi sababu hakuamini kama alipona.Mbali na hapo hakutaka tena kubaki nchini Marekani alitaka kurejea Tanzania mara moja,hicho ndicho kitu kilichotokea Nasra akatafutiwa tiketi na gharama zote zikawa juu ya ubalozi wa Tanzania nchini humo.

******

Kifo cha ugonjwa wa ukimwi jinsi kinavyouwa vibaya ndiyo kilikuwa kinamuumiza kila kukicha,Alex alikosa raha ya maisha na kutokana na kuwaza sana ilimfanya mpaka usiku awe anaota njozi mbaya zilizozidi kumtisha zaidi,mawazo yalikula ubongo wake akapungua uzito, mke wake alilijua hilo na kujaribu kumfanya asiwaze lakini haikusaidia,Alex aliwaza mambo mengi na hata ilipofika usiku kuanzia aambiwe ana virusi vya ukimwi hakutaka kushiriki na mke wake tendo la ndoa.
“Baby usijali,Please leo nina hamu nawewe”
“Latifah sitaki kukuuwa”
“Tutatumia kondomu”
“Naomba unielewe mke wangu,sitaki ufe kama nitakavyokuja kufa.Naelewa nini maana ya ugonjwa huu.Tafadhali sana”
Latifah alikuwa amevaa nguo ya kulalia peke yake, mapaja yake yapo wazi na kile alichovaa ndani kilionekana,damu yake ilimuenda mbio alitamani kufanya ngono na mume wake,Alex.
“Hata kama Latifah mimi siwezi”
Hakutaka kumuuwa mke wangu na ugonjwa huo hatari ingawa aliamini kwamba kondomu inazuia virusi vya ukimwi lakini hakuipa asilimia zote mia moja,alimtizama mke wake jinsi alivyokuwa mzuri mwenye macho ya kipole na kutamani siku zirudi nyuma ili abadilishe mambo lakini haikuwezekana,alizidi kumuangalia mke wake machoni na kuona ni jinsi gani alivyokuwa na penzi la ukweli,isingekuwa rahisi kwa mwanamke yoyote yule kuambiwa mume wake ana virusi vya ukimwi na akakubali kuishi naye achilia mbali kushiriki naye tendo la ndoa,moyo wa mwanamke huyu ulikuwa wa ajabu sana.
“Alex usilie mume wangu”
Machozi yaliyokuwa yanamlenga Alex yakaanza kumtoka,mkewe akamsogeza karibu na kumpiga piga mgongoni ilikuwa ni picha ya kuuzunisha kwa wanandoa hawa.
“Naom..ba unisa..mehe Mke wangu.Nimeamini unanipenda sana,natamani siku zirudi nyuma nirekebishe yaliyotokea la..kini haiwezekani tena”
“Usiseme hivyo Mume wangu,wapo wengi wenye matatizo kama yako”
“Hapana Latifah usinipe moyo,nakuonea huruma sana kukuacha Mwanamke Mjane,naomba nisimame kidogo”
Alex alitoka kitandani na kwenda mpaka kwenye kabati hapohapo akavuta droo na kutoa faili lililokuwa na makaratasi,bado Latifah hakuelewa nini maana yake,akachukuwa peni akawa kama anaandika juu ya karatasi baada ya kumaliza akatia sahihi.
“Nikifa usije ukasumbuliwa na ndugu zangu,kila kitu kipo humu utamuona Mwanasheria anayeitwa Sudi Iserre”
“Al..”
“Latifah naomba unielewe”
Kila kilichoongelewa na Alex kilimuogopesha mkewe na alielewa nini maana ya maneno hayo kutoka kwa Alex,hakutaka kuamini kuwa mume wake amekata tamaa tayari ya kuishi.Latifah alitumia usiku mzima kumpa moyo Mume wake lakini ikawa ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa acheze!
***
Siku iliyofuata Alex aliamka mapema sana akaingia bafuni na kuoga,hakuwa na uhakika kama atarudi siku hiyo.
“Unaenda wapi mapema yote hii Darling?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Mkewe akiwa kitandani bado,ilikuwa ni asubuhi ya saa kumi na moja.
“Nimepigiwa simu leo niwahi ofisini”
“Saa ngapi?wakati tulikuwa wote,sikusikia ukipigiwa si…”
“Nina kikao mke wangu naomba nielewe”
“Sawa”
Alex baada ya kuchomekea vizuri akavaa koti na kutoa bastola yake,akaiangalia kwa kitambo na kuiweka kiunoni.
“Alex”
“Naam”
“Naomba uiache hiyo bastola”
“Unadhani nitajiua?”
“Tafadhali nakuomba”
“Usijali mke wangu”
Alex alijibu huku akitembea na kutoka chumbani,akatembea mpaka seblen ambapo aliitizama nyumba yake mara mbilimbili,hakuamini kwamba ataenda kuacha mali zake zote.Aliwakumbuka watoto wake wadogo Jamal na Mackline ambao walihitaji mapenzi ya baba yao.
Hakutaka kupoteza muda akatembea mpaka nje na kuingia ndani ya gari lake akaliwasha,tayari kwa kulitoa nje.
“Pipipiiiiiii”
Mlinzi alivyosikia honi akaruka kutoka kwenye kiti na kufungua geti,gari la tajiri yake likatoka nje kwa kasi isiyo ya kawaida.
Sura ya Sonia ndiyo iliyomjia kichwani mwake na hakuelewa amfanye nini mwanamke huyu Malaya asiyekuwa na adabu.
“No Hafuan,huwezi kupona lazima tufe wote”
Alex aliendesha gari na kuchomoa bastola yake akaiweka kiti cha pembeni,safari yake ilikuwa ni Mikocheni B kwa Sonia kwa nia ya kumfanya kitu chochote kile kibaya ikiwezekana amfyatue risasi amuuwe.

Baada ya dakika ishirini alikuwa Mikocheni B ameweka gari karibu na ukuta wa nyumba ya Sonia akiwa anamsubiri atokeze, aliamini kuwa akifika getini asingeweza kuruhusiwa kuingia ndani na walinzi ndiyo maana akawa anamsubiri nje,hakukaa sana akaona taxi imesimama nje ya geti lake.Akazidi kupandwa na hasira alivyomuona Sonia anashuka na kumlipa dereva pesa yake.
“Usijali mzee alishalipa”
Dereva taxi alimwambia Sonia alivyotaka kumpa pesa yake.
“Kumbe alikulipa?”
“Ndio”
“Sawa”
Sonia alilala na Mzee Stanley Mwandambo usiku kucha na alirudi asubuhi yake,akaingia ndani ya geti na kunyoosha mpaka ndani kwake.Bila kufanya chochote akajitupa kitandani.
‘VIZA YAKO TAYARI, KAICHUKUWE IJUMAA CODE 114K5R UKIIPATA NAOMBA UNIAMBIE”
Ulikuwa ni ujumbe wa meseji ukitokea nchini Marekani kutoka kwa Mama yake,Pendo Jonas. Alivyofungua ujumbe mwingine alishtuka.
‘SONIA NAOMBA UNISAMEHE NIMEANDIKA MESEJI HII KWA MAJUTO MAKUBWA SANA,NINA IMANI ULINIPENDA LAKINI NI TAMAA ZANGU ZA MWILI ZILINIPONZA NIMEAMUA KUKWAMBIA UKWELI SABABU NINAVYOONGEA SASA HIVI SIJUI NITAISHI VIPI,SONIA NAOMBA UKAPIME VIRUSI VYA UKIMWI,NAOMBA UNISAMEHE SANA KWANI SIKUJUA,NILIAMBUKIZWA NA MWANAMKE ANAYEITWA SAMIA BILA KUJIJUA NA NINA AMINI KUWA MIMI NILIKUPA WEWE BILA KUELEWA.NAELEWA KWAMBA BINADAMU TUNASTAILI KUSAMEHEWA PALE TUNAPOKOSEA LAKINI HILI SIDHANI KAMA ITAKUWA RAHISI KUNISAMEHE,SIKATAI NILIKUPENDA SANA.HIVI NINAVYOONGEA NAWEWE TAYARI NIMEANZA DOZI YA ARV,SINA UHAKIKA KAMA NITAPONA'
Alihisi moyo wake unamuuma sana baada ya kugundua kuwa Partson ndiye aliyempa ugonjwa wa Ukimwi,alilia kwa kudhani wenda Leythan ndiye aliyemuambukiza ukimwi alimuhurumia mwanaume huyo sababu hakuwa na hatia.
“No!”
Kuna kitu kilimjia kichwani ghafla hapohapo,mimba aliyokuwa nayo ilimvuruga akili.Alimuomba Mungu msamaha kwa hatua anayotaka kuichukuwa kwa wakati huo,ilikuwa ni lazima aitoe hakutaka kuzaa mtoto mwenye ugonjwa wa Ukimwi na baadaye aje kuteseka duniani.Hapohapo akaingia bafuni akajimwagia maji,akachukua elfu hamsini kwenye pochi na kutoka nje.
Kabla ya kutoka nje ya geti alitafakari kidogo kabla ya kutaka kufanya maamuzi anayotaka kufanya.
“Eh Mungu naomba nisamehe,najua nimefanya dhambi nyingi lakini hii nina Imani ni kubwa”
Sonia alijisemea na kutoka nje ya geti,akielekea duka la madawa ili atafute vidonge vya majira atoe mimba iliyotokana na kubakwa,umbali kutoka nyumbani kwake mpaka duka la madawa ulikuwa ni kama mita kumi hivi,ilikuwa ni asubuhi sana kwa maana hiyo hakuwa na uhakika kama angekuta duka la madawa lipo wazi.
Alitembea akiwa na mawazo na kilichomshtua ni mkono wa mtu kumgusa begani,alivyogeuka alijikuta ameshtuka sababu hakutegemea kumuona Alex kwa wakati huo.
“Tulia hivyo hivyo,ukipiga kelele utakuwa mwisho wako”
Alex alichomoa bastola,akamshika Sonia mkono akaingia naye ndani ya gari.
“Alex unataka kufanya nini?unanipeleka wapi?”
“Nyamaza Malaya”
Gari lilizidi kutembea kwa kasi,Alex akashindwa kuelewa amfanye nini mwanamke huyu Sonia.
“Laki..”
“Nyamaza,Chagudoa wewe leo ndio utanieleza mimi ndiyo nani”
Gari lilizidi kutoka kwa kasi ya ajabu, Alex alikunja kona ya kuelekea chuo kikuu UDSM kwa kasi ya ajabu,kutokana na kuwa asubuhi sana hakukuwa na msongamano mkubwa wa magari.Akazidi kuingia ndani ndani na kukunja kushoto baada ya kufika sehemu yenye mitimiti mingi aliweka gari kando,akazunguka upande wa pili na kufungua mlango.
“Shuka Malaya,Shuka upesi”
Alex alibanwa na hasira bastola yake ikiwa mkononi,akatizama huku na kule akafungua boneti la gari akatoa kamba,akamvuta Sonia mpaka mtini.Akamfunga kamba mwili mzima.
“Wewe Malaya,kwanini umeniua lakini?”
“Nakuuliza wewe Changudoa Malaya Mbwa”
Sonia alimtizama Alex kwa nyodo,hapohapo alipokea ukofi, akapigwa ngumi ya uso, mdomo wake ukapasuka,damu zikaanza kumtoka.
“NDIO NIMEKUPA UKIMWI ALEX,NDIO NIMEKUPA UKIMWI,KWANINI HUKUTULIA KWENYE NDOA YAKO?BABA YAKO NDIYO KATAKA YOTE”
Sonia alipandisha hasira hapohapo akapigwa kofi lingine,tayari ngozi yake ilibadilika rangi na kuwa nyekundu.
“Hafuan,Hafuaaaaan.Kacha kacha”
Alex akakoki bastola na alidhamiria kumuuwa Sonia hapohapo mtini kisha nayeye ajiue.Alimtizama mwanamke huyo mara mbili mbili na kutamani kummeza mzimamzima.
Kidole chake kilikuwa tayari kinasogea kwenye triga kumaanisha kuwa risasi itoke na kupasua kichwa cha Sonia aliyekuwa mtini.
“Hata ukiniua ni kazi bure tu”
“Unasema nini?”
“Kama ulivyonisikia,tena fanya haraka ili unipunguzie mateso nitakayoenda kukutana nayo mbeleni”
“Kaaa kimnya”
Alex alihisi kumuuwa Sonia kwa kumpiga risasi haitosaidia alitaka nayeye apate shida kabla ya kifo chake,bila kuongea chochote aliingia ndani ya gari akalirudisha nyuma na kuondoka zake.

Sonia alibaki mtini na kutoelewa Alex ana maana gani na alipofungwa haikuwa rahisi kwa mtu yoyote kumuona, alikuwa ndani ya miti na njia hiyo ilikuwa nadra kwa watu kukatiza,masaa matano yalivyopita alianza kuhisi njaa inakwangua tumbo lake,miguu ilimuuma.
Mateso hayakuishia hapo ilifika usiku akiwa hapohapo mtini alihisi kuishiwa nguvu mwilini lakini alikuwa akijipa moyo kuwa atapata msaada.Aliendelea kusubiri mpaka kunakucha na siku iliyofuata ilikuwa hivyohivyo.Kilichomshtua usiku wa pili yake tangu afungwe kamba ni taa za gari,kwa kuwa zilimmulika machoni ilikuwa tabu kujua ni nani.
“Wewe Malaya bado upo hai?”
Hapo ndipo alipogundua kuwa ni Alex tena akiwa na bastola mkononi.Alex hakwenda kumuona Sonia bali kumuuwa na huo ndiyo uamuzi aliouona ni sahihi.
Alikagua bastola yake na kuchukizwa baada ya kukuta ina risasi moja peke yake nia yake ikiwa nayeye ajiuwe pia.Akaingia ndani ya gari na kulirudisha nyuma kwa kasi,akaweka gia na kulitoa mbio ikiwa ni kwenda kumgonga Sonia mtini.
****
Mlio wa bastola kufyatuliwa ndiyo iliwafanya polisi waliokuwa doria washtuke,walikuwa kama mita mia saba hivi,wote wakashika bastola zao vizuri kujihami, hakuna hata askari mmoja aliyejuwa mlio huo umetokewa upande gani,ndio maana wakatulia kidogo.
“Afande umesikia hiyo?”
Askari aliyekuwa anaendesha gari alimuuliza mwenzake.
“Ndiyo ni mlio wa risasi huo”
“Ni wapi hiyo itakuwa?”
“Upande wa Magharibi kule, kuna umuhimu wa kuchoma mafuta kwenda?”
“Sidhani,embu tusubiri kwanza”
Askari wote wakapuuzia hawakutaka kuchoma mafuta yao kujisumbua kutokana na mlio huo kusikika mara moja.
****
Kilichowashangaza wanafunzi wa chuo ni harufu kali na kunguru wengi,hawakuelewa ni kitu gani kinatoa harufu kali kiasi hicho na kuwaumiza pua.Ilibidi uongozi wa Chuo ufuatilie swala hilo ndipo wakaamua kuingia porini,kila mtu alipigwa na butwaa,walichoona kiliwatisha ilikuwa ni maiti ya mwanamke imegongwa na gari mtini na kwa mbali ilianza kuoza ndiyo maana ilitoa harufu kali sana!Ndani ya gari pia kulikuwa na mtu amepasuka kichwa kwa risasi ubongo upo nje,eneo hilo lilinuka damu.Hapohapo askari waliitwa hata wao walishangazwa sana,maiti za watu hao ziliwatisha kupita kiasi walivyojaribu kuunganisha chanzo cha tukio lililotokea hawakupata jibu kamili,kila mtu alishindwa kutegua kitendawili cha maiti hizo mbili.
***
Msiba wa Sonia ulisikitisha watu wengi sana sababu habari za kifo hicho kilitangazwa vyombo vya habari mbalimbali,Leythan aliyekuwa gerezani aliumia moyo baada ya kuona gazeti lenye picha ya Sonia na pembeni ikiwepo picha akiwa amegongwa na gari yupo mtini,Partson Ngogo ndiyo usiseme!Siku hiyo alilidondosha machozi akiwa hospitalini anasubiri dawa za ARV.
Msiba ulisafirishwa mpaka mkoani Kilimanjaro,kwa ajili ya maziko.Walisikitika zaidi baada ya kupokea msiba mwingine wa Brenda,likawa pigo jingine kubwa sana mtu na dada yake kufa kwa kipindi kimoja.Nasra alilia kupita maelezo yaliyojitosheleza hasa alipogundua kuwa Marehemu Brenda pia ni ndugu yake.
“Soniaaaaa,Ndugu yanguuu eeeh Mungu wangu Brenda mdogo wangu naw..ewe umekwen..da”
Nasra aliangua kilio pembeni akiwa ameshikiliwa na Mchumba wake Captain Mustapha,ulikuwa ni uzuni mkubwa mno.
Baada ya siku arobani kupita walianua matanga na Wazee wa Kichaga akiwemo Mzee Shayo wakaaka vikao wakaamua kuwa mali alizoacha Sonia akabidhiwe Nasra,hilo halikuwa na tatizo.
****
Kutokana na ugonjwa uliowauwa ndugu zake, Nasra na Mustapha ilikuwa kila mwisho wa mwezi wanaenda kutembelea wagonjwa wenye maambukizi ya ukimwi.Na Kila ilipofika tarehe kumi na tano mwezi wa saba,walifunga safari na kwenda Mkoani Moshi kuangalia makaburi ya Sonia na Brenda, walizikwa karibu kabisa na makaburi ya wazazi wao,Marehemu Nickson na Gloria!

** ***MWISHO*****



UJUMBE;
Huwezi kumgundua mtu mwenye
maambukizi ya ukimwi kwa kumwangalia kwa macho.Ukimwi upo na unaua,hasa vijana,ni vema kujua afya ya mwenzako kabla ya kujiingiza katika masuala ya kimapenzi.Epuka ngono zembe!
USIKOSE KUWA SAMBAMBA NA MTUNZI EMMANUEL F. KWAY KATIKA HADITHI NYINGINE INAYOKWENDA KWA JINA LA ‘BEDROOM PROFESSIONALS ’


*******
ENDELEA KUSOMA HADITHI NA SIMULIZI ZA MTUNZI….EMMANUEL F.KWAY(THE STORY MASTER)

0 comments:

Post a Comment

BLOG