Search This Blog

Sunday, May 31, 2020

BEDROOM PROFESSIONALS SEHEMU YA 5/10



BEDROOM PROFESSIONALS
MTUNZI….EMMANUEL F.KWAY(THE STORY MASTER)
AGE…(18+)
WatsApp…+255718 862176
SEHEMU YA 5 KATI YA 10 MWISHO
*******


Deo alisota maabusu mpaka kunakucha bila mtu yoyote yule kumuona,hakuelewa ni kwanini
ameshikiliwa kwa kosa lisilokuwa lake.Tangu azaliwe hakuwahi kufanya biashara haramu hata siku moja,swala la kukutwa na madawa ya kulevya ndani ya mfuko wake lilimshtua kupita kiasi na kitendo cha kutokuona Passpot yake ndilo lilimchanganya akili yake kwa kiasi cha kutosha na kilichomvuruga kabisa mpaka siku inayofuata hakuna mtu yoyote aliyeenda kumuangalia kituo cha polisi,sio Amadour wala mke wake.
Usiku mwingine ukaingia lakini wapi,hakukuwa na dalili yoyote ile.Ingawa maabusu ilikuwa safi ina kitanda kizuri chenye mashuka masafi lakini aliumia mtima sababu wakati kama huo ilitakiwa awe na familia yake akifurahia maisha jijini Paris!Askari walimpelekea chakula lakini hakujisikia hamu yoyote ile ya kula, alichotaka yeye azungumze na mwenyeji wake anayeitwa Amadour.
“Please officer call Amadour”(Tafadhali afande mpigie Amadour)
“Shut up”(Kimnya)
Askari akapiga mkwara hiyo ilimfanya Deo anyong’onyee!Alielewa maana yake kwa kosa la kukutwa na madawa hayo haramu ya kulevya,alilia na kusikitika sana sababu angeenda kufa kwa kosa la kupakaziwa!
*********
Mpango wa Amadour ulikuwa tayari umetimia,hakuna kosa kubwa alilofanya Marietha kama kusema kwamba Mume wake ni muuza madawa ya kulevya!Ilikuwa sio kwa matakwa yake bali ni Shinikizo la Amadour, hakuelewa kwamba amejiingiza katika hatari mbaya mno.Amadour alijifanya kuwa bega kwa bega na Marietha akijifanya ameguswa na kwamba anaenda kumuona Deo rumande kila kukicha,kumbe haikuwa hivyo.Alikuwa ana mahesabu yake makali kichwani,kila kilichotokea kwa Deo mpaka akawekwa ‘lockup’ yeye ndiye alikuwa mkandarasi.Aliamini jambo analofanya sio sahihi hata kidogo lakini hakujali hata kidogo,ilikuwa ni lazima afanye ngono na Marietha tena sio chini ya Mara moja au mbili ili Deo awe huru,hayo ndiyo yalikuwa mahesabu yake,kwa jinsi alivyopanga mpango huo alijiona yeye bingwa na kudiriki kujiita Chuck Noris.
“Mimi ndio Chuck Noris,lazima huyu mrembo apigwe dudu.Lazima nisafishe rungu,kiulaiinii”
Siku hiyo Amadour aliwaza akiwa ana kipande cha fegi mkononi mwake,anapuliza moshi hewani.Mawazo yake yote yalikuwa kwa Marietha,alijaribu kumvua nguo kihisia na kumuona ni jinsi gani alivyokuwa mzuri wa kuvutia!
Hakutaka kupoteza mida,usiku wa siku hiyo akaibuka hotelini na kumkuta Marietha yupo chumbani kwenye kona ya kitanda,ameinama analengwa na machozi.
“Amadour,afadhali umekuja!Vipi hali ya Mume wangu?”
Hilo ndilo swali la kwanza kulitupa Marietha akidhani kwamba Amadour yupo upande wake.
“Nimetoka kumuona”
“Imekuaje?”
“Mambo bado magumu”
“Kwanini?Tafadhali naomba unisadie”
“Nitakusaidia lakini nawewe inabidi ujiongeze”
“Kivipi?Kuna nini?Nikupe pesa?”
“Hapana”
“Nini sasa?”
“Kwanza nasikitika kukwambia kwamba Mumeo kesho atanyongwa lakini maisha yake yapo mikononi mwako mwenyewe”
“Amadour”
“Inabidi nilale nawewe leo ili Deo atoke”
Amadour hakutaka kupindisha maneno,akaweka kila kitu wazi.Kauli hiyo ilimshtua sana Marietha!



“If you want them to release him you have to sleep with me.I will help,you should also do the same thing.Unless otherwise your husband is a deadman”(Kama unataka awe huru inabidi ulale na mimi,nakusaidia nawewe nisaidie.Vinginevyo mumeo ni mfu)
Hiyo ndiyo ilikuwa kauli kutoka kwa Amadour akimwambia Marietha wakiwa chumbani.Marietha alikuwa ni mwanamke anayejiheshimu, haikuwezekana hata siku moja kuvua nguo yake ya ndani na kuipanua miguu yake na kufanya ngono na mwanaume mwingine isipokuwa mumewe, Deo!Hiko ndicho kitu alichoapia kukifanya.Alijaribu kumtafakari Amadour na kushindwa kummaliza,alihisi kuchoka akili mpaka mwili mzima.Uhai wa Deo ulikuwa mikononi mwake mwenyewe!
“No,I can’t”(Hapana siwezi)
Marietha aliropoka lakini hakuelewa kama amechukuwa maamuzi sahihi,alivyomuangalia mwanaye Abraham alihisi kuumia moyo!
“Okay!But remember,I’m innocent”(Sawa,lakini kumbuka sina hatia)
Amadour alijibu kwa dharau kisha akatoa kadi yake ya mawasiliano na kuitupa kitandani.
“Just incase you will change your mind.Contact me”(Ikitokea umebadili maamuzi yako tuwasiliane)
“One more thing….you have few hours to decide”
Amadour akaongeza neno lingine baada ya kufika mlangoni kisha kuondoka zake.Bado Marietha alishindwa kuelewa alimkosea nini Mungu wake,akachukuwa muda mchache uliobaki kusali na kumuombea mumewe sababu hakuwa na tumaini lingine zaidi,kuvua nguo yake ya ndani na kufanya ngono na Amadour aliamini kwamba ulikuwa ni usaliti mkubwa sana katika ndoa yake na asingeweza kusahau hata kidogo na bila kufanya hivyo basi Deo angeuwawa kwa kunyongwa, alivyowaza kitu kama hicho moyo ulimuuma ajabu kwa maana hiyo maisha ya Deo yalikuwa mikononi mwake mwenyewe,ilikuwa ni lazima achague kusuka ama kunyoa.
“Eeh Mungu wangu nimekukosea nini?Kwanini mimi?”
Marietha alijaribu kuteta na Mungu wake lakini hakupewa jibu ni kitu gani akifanye,masaa siku hiyo yalienda harakaharaka kupita kiasi.
“Deo ninafanya hivi kwa ajili yako,Mungu naomba unisamehe sababu nampenda Mume wangu”
Hiyo ilimaanisha kwamba anataka Deo awe hai kivyovyote vile ilikuwa ni lazima afanye tendo la kuzini na Amadour,bila kujifikiria tena kwa mara nyingine akachukuwa kadi iliyokuwa kitandani na kuiendea simu ya mezani,akaanza kumtafuta Amadour hewani, ilivyopokelewa akajitambulisha.
“Kwahiyo umekubali?”
Hilo ndilo swali la kwanza kulitupa Amadour.
“Amadour,hakuna njia nyingine yoyote ile?”
“Hapana”
“Sawa”
“Kwahiyo umekubali?”
Kukataa alitaka lakini alishindwa badala yake machozi yakawa yanambubujika.
“Hallooo”
Amadour akamuongelesha tena.
“Nd….io”
Marietha akasema kwa uchungu na kuweka mkonga wa simu mezani,machozi yalimtoka na alielewa baada ya dakika chache atakuwa kitandani na Amadour wanafanya ngono,tendo hilo kwake alilifananisha na ubakaji kwasababu haikuwa kwa ridhaa yake.Dakika tano baadaye simu ya mezani ikaita na ilitoka mapokezi,Amadour alikuwa tayari ameshafika moyo wa Marietha ulizidi kupiga kwa nguvu lakini hakuwa na jinsi akakubali aruhusiwe,hivyo ndivyo ilivyokuwa Amadour hakupoteza wakati akawa keshafika mlangoni na kuanza kugonga,Marietha akafungua.
“Ahsante”Amadour akashukuru.
Bado Marietha hakuamini kwamba mwanaume aliyekuwa mbele yake alitaka rushwa ya ngono,alitamani siku zirudi nyuma akatae safari ya Paris lakini haikuwezekana hata kidogo ilikuwa ni lazima alale na Amadour tena wafanye ngono.
“Tusipoteze wakati”
Amadour akashauri baada ya kuingia chumbani alijiona yupo sahihi kabisa kufanya kitu kama hiko,kufanya ngono na Marietha kwake ilikuwa kama ndoto ilikuwa ni lazima itimie.
“Amadour”
Marietha akaita kwa sauti ya huruma.
“Tufanyie hapahapa au?”
“Hapana,kuna mtoto”
“Sawa,ngoja nikatafute chumba kingine”
Amadour hakupinga kauli ya Marietha alijuwa kivyovyote vile ni lazima afanye ngono hata iweje.Ni kweli hakuwa na masihara alienda mpaka mapokezi na kuomba chumba kingine,akapata na kurudi chumbani kwa Marietha.
Bado alishindwa kuelewa jambo hilo ni ndoto au kweli,alikuwa nyuma ya Amadour wanaongozana mpaka walipofika nje ya mlango wa chumba kingine na kufungua,Amadour akaingia Marietha akafuata.Kitu kilichokuwa kinataka kuendelea hakuna mtu yoyote aliyekuwa hajui kati yao,Amadour akavua shati akabaki kifua wazi mwili wake ulikuwa umejaa michoro ya ‘tatou’hakutofautishwa na gazeti,akatembea mpaka mlangoni na kutia ‘lock’ akamsogelea Marietha karibu na kumshika kidevu na kuanza kumnyonya mdomo,hakuwa na muda wa kuvua nguo ya juu ya Marietha aliichana kama kipande cha karatasi sababu alikuwa ana mori ya kufanya ngono,Marietha alizidi kutetemeka akahisi kama uti wake wa mgongo umepigwa na ubaridi.
“Una condom?”
Marietha akahoji.Ni sawa alikuwa yupo tayari kufanya ngono lakini pia alitaka kujikinga na magonjwa ya zinaa.
“Sina”
“Katafute Condom”
“Huo muda sina,kama hutaki mumeo atanyongwa na kufa lala chali”
Marietha akasukumizwa kitandani na nguo zake zikawa zinavuliwa,kilichofuata hapo ni Amadour kuvua nguo zake harakaharaka,akashika mashine yake vizuri na kuipanua miguu ya Marietha na kuingiza.Kitendo alichofanyiwa Marietha kilikuwa ni cha kinyama na hakikuweza kusemeka wala kuandikwa kwenye kalamu na karatasi,unyama huo hakuweza kuufananisha na kitu chochote kile duniani na aliapia kwamba atabaki na siri hiyo mpaka anafukiwa kaburini.Japokuwa Amadour alikuwa juu ya kifua chake anafanya naye ngono lakini akili yake haikuwa hapo hata kidogo,alikuwa akifikiria vitu vingi sana na endapo Deo akitoka mahabusu ilikuwa ni lazima warudi Tanzania.
“Aaaaaaaaah”
Amadour ndiye alikuwa akimaliza mzunguko wake wa kwanza,akalala kifuani kwa Marietha,alijisikia mwepesi.Uchungu aliohisi moyoni haukuwa na kipimo chake,akamsogeza Amadour pembeni na kuvuta shuka.
“Wewe ni mtamu sana,Mumeo anafaidi mno”
Amadour akamwaga sifa hakuelewa ni kiasi gani anazidi kuuchoma moyo wa Marietha.
“Nataka kumuona Deo”
“Sawa”
“Sasa hivi”
“Hapana,bado nina kiu”
Hiyo haikuwa utani.Baada ya dakika tano Mashine ya Amadour ilisimama upya akamgeuza Marietha na kuanza kufanya ushenzi wake tena bila kumuandaa,mgodi wa Marietha ulikuwa mkavu hiyo ilimfanya aumie na achubuke lakini haikumfanya Amadour asitishe kufanya anachokifanya.Mpaka anaridhika ilikuwa imetimu saa tatu za usiku!
******************
“Hapana mimi siuzi madawa ya kulevya”
“Unafanya biashara gani?”
“Nina maduka ya vifaa vya ujenzi”
“Taifa lako?”
“Tanzania”
“Passport yako iko wapi?”
“Nilikuwa nayo ndani ya gari lakini siioni”
“Hapana huna passpot,umeingia kinyemela nchini”
“Ninayo na nimeingia Alhamisi kihalali,angalieni uhamiaji”
“Wewe ni muuza madawa ya kulevya”
“Siuzi madawa ya kulevya”
“Unauza,usibishe kubali.Taja wenzako.Unajuwa hukumu yake?”
“Mimi siuzi madawa ya kulevya,naomba niongee na ubalozi wa Tanzania”
Deo alikuwa msomi na alijibu maswali bila kutetereka,ni wazi kwamba alijuwa anasingiziwa ndio maana hata maaskari wenyewe walionekana kuhaha.
“Unamfahamu Marietha?”
“Ndio”
“Ni nani yako?”
“Mke wangu”
Askari mmoja akasimama kutoka ndani ya chumba cha mahojiano na kutoka nje,baada ya dakika moja akarejea na kinasa sauti na kukiweka mezani!
“NDIO ANAUZA MADAWA YA KULEVYA,NI MUME WANGU”
Deo hakutaka kuamini kwamba Marietha ndiye ametamka maneno hayo.Alibaki akiwatizama maaskari.
“Hii sauti unaitambua?”
Askari akauliza.
Bado ilikuwa vigumu kwa Deo kujibu,wakaiweka tena,sauti ikaenea chumba kizima.
“Huu ni ushahidi tosha kwamba wewe ni muuza madawa ya kulevya,hata hivyo mkeo ametia sahihi hapa kuwa ni kweli unauza madawa ya kulevya”
Deo aliitizama karatasi na chini kulikuwa na sahihi ya mkewe.Akakusanya matukio mbalimbali na kuunga unga kila kitu,Amadour hakuonekana wala mke wake hiyo ilimfanya aanze kuhisi kuna kitu kinaendelea tena kisichokuwa cha kawaida.Alimuomba Mungu sana isiwe kama anavyofikiria!
“Sio kweli hapana Marietha,usinifanyie hivyo”
Kitu alichohisi Deo ni kuwa Marietha ndiye aliyemuwekea madawa ya kulevya na hakuna mtu mwingine ambaye angefanya kitu kama hiko ingawa hakujuwa ana hila gani!
“Marietha kwanini umenifanyia hivi?”
Deo aliwaza na kumuhukumu moja kwa moja mkewe, Marietha!



Bado hakutaka kuamini kwamba Marietha ndiye aliyemuwekea madawa ya kulevya ili afungwe na baadaye anyongwe na kutoweka duniani,tena akiwa ughaibuni! Moyo wake ulimuuma kupita kiasi hasa alivyokumbuka mapendo aliyomuonesha.Vitu vingi sana vikawa vinamiminika kichwani mwake kama maji akawa kama anaangalia mkanda wa sinema,akajiona akiwa kanisani anakula kiapo kwamba watakuwa mwili mmoja.
“Wewe ni muuza madawa ya kulevya,kubali”
Ilionekana askari walitaka Deo akubali kauli hiyo ili ripoti yao ikamilike.
“Nahitaji kuongea na ubalozi wa Tanzania.Sitoongea chochote bila mwanasheria”
Ilibidi askari wote waangaliane.
**********
Tayari ndoto yake ilikuwa imetimia bado hakuamini kama amefanya ngono na Marietha tena kiulaini bila hata kutumia nguvu yoyote ile,bado alikuwa kitandani Marietha yu pembeni yake analia machozi.Marietha alihisi kujuta kwa kitendo alichokuwa amekifanya lakini nafsi nyingine ilimpa moyo ikimwambia kwamba alifanya hivyo ili kuyaokoa maisha ya mumewe na wala si vinginevyo,kwa kitu alichokifanya alijiona kama yupo juu ya televisheni kubwa na dunia nzima inamtizama, alijisikia aibu kupita kiasi na wakati mwingine alitamani asingezaliwa mwanamke,mateso aliyopitia ilitosha kabisa kumdhiaki Mungu wake!
“Na..omba niongee na Deoo”
Marietha aliongea kwa kwikwi na hasira,alitamani achukuwe kisu amuuwe Amadour hapohapo lakini hakukuwa na uwezo wowote ule!Amadour hakuwa ana habari yoyote ile,kile alichokifanya alikiona ni kitu cha kawaida kwake,akapeleka mkono wake chini na kuvuta koti lake ambapo alitoa pakiti ya sigara na kiberiti akawasha na kuanza kupuliza moshi kutokea puani.
“Nataka kumuona Deo”
Marietha alizungumza tena.
“Deo?”
“Ndio”
“Sasa hivi huoni ni usiku?”
“Hata kama”
“Haitowezekana”
Ulikuwa ni usiku mnene tayari lakini Marietha hakutaka kukubali,alishikilia msimamo wake kwamba anahitaji kuonana na Deo lakini ikawa ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa kwani Amadour aliendelea kupuliza moshi hewani kwa dharau.
“Nimekwambia sasa hivi ni usiku,usinisumbue”
Marietha alimwaga machozi,msaada alioutegemea na kutoa rushwa ya ngono aliona kama kazi bure kwake!Hakuna kitu alichofanya kingine zaidi ya kusimama na kutoka kitandani na kuvaa nguo zake,alitoka huku akilia kwa hasira, hakuelewa ni kwa njia gani apate msaada sababu alikuwa mgeni wa jiji.
Akatembea na kutafuta mlango wa chumba chake, huko alimkuta mtoto wake Abraham analia,akatembea taratibu mpaka kitandani!Alivyomuangalia Abraham kwa umakini sura ya mume wake Deo ilimpitia kichwani na alijiona ni msaliti na pia mkosaji mbele za Mungu wake aliye juu Mbinguni.
“Eh..Mungu wangu,niambie ni kosa gani nimelifanya?”
Uchungu ulimbana hakuweza kuufananisha na kitu chochote kile.Furaha yote tayari ilibadilika na kuwa shubiri alijihisi kujuta sana,mambo yaliyokuwa yanamkabili yalikuwa mazito kupita kiasi mpaka akadiriki kusema kwamba ni bora afe kuliko kuendelea kupata mateso na kudhalilishwa namna hiyo ndani ya ndoa yake,alijuwa sana kwa kusema hayo yote alikuwa ana mkufukuru Mungu.
Mtumishi wa Mungu kama yeye alipaswa kupiga goti na kusema asante Mungu kwa kila kitu na kuchukulia mambo yanayotokea ni kama changamoto za duniani na ipo siku atashinda lakini haikuwa hivyo kwake!
“Hata Mungu ungekuwa wewe ndiyo mimi ungefanya nini?”
Akajikuta ameropoka bila kutarajia.Siku hiyo hakupata usingizi alimnyonyesha Abraham na kulivyokucha akasimama na kuingia bafuni kujimwagia maji,bado hakutaka kuamini kwamba dunia imempa kisogo na kila kitu kiligeuka na kuwa chini- juu.
Alijimwagia maji na kurudi chumbani,akavaa nguo na kukaa kitako kitandani!
***************
Deo aliendelea kushikilia msimamo wake kwamba hakuhusika na utumiaji wa madawa ya kulevya na badala yake alitaka kuzungumza na ubalozi wa Tanzania,hapo ndipo maaskari walipoanza kuchanganyikiwa.Ukweli ni kwamba zilikuwa ni njama walizochonga na Amadour,kila askari alikula shilling dola mia moja ili wamuweke ndani Deo Karekezi,waliamini wanaenda kinyume na sheria lakini hawakujali hilo, kwao pesa ilikuwa mbele kama tai,ndiyo maana wakadiriki kumpakazia Deo kesi ya madawa ya kulevya.Waliamini kwamba mambo yangeenda kiulaini lakini jambo lililokuwa linaenda kutokea mbeleni waliliogopa kupita kiasi,walivyosikia Deo anahitaji mtu kutoka ubalozi wa Tanzania ndipo walianza kuhaha.
“Unataka mtu wa ubalozi ili iweje?Kesho utanyongwa kenge wewe”
Askari alifoka siku hiyo akijaribu kumpiga Deo mkwara ili asizungumzie habari za ubalozi wa Tanzania.
“Sawa nitanyongwa nitakufa,kabla ya ninyi kufanya kitu hiko naomba niongee na ubalozi wa Tanzania.Na hamuwezi kuninyonga bila nchi yangu kujuwa nataka swala hili mlitangaze vyombo vyote vya habari kuwa mnataka kuninyonga”
“Wewe unatoa kauli hiyo kama nani?Nakuuliza wewe.Tena unyamaze”
“Siwezi kunyamaza,nahitaji kuongea na ubalozi wa Tanzania.Mimi ni mtanzania naomba swala hili ubalozi ujuwe”
Siku hiyo polisi waligongana vikumbo,majasho yaliwatoka Deo alichachamaa na aliongea kwa hasira kupita kiasi,swala la yeye kusingiziwa ndilo lililomuuma hata kama angenyongwa kwa kupigwa kitanzi alitaka swala hilo lijulikane Tanzania nzima na aliamini kwa sheria za dunia ilikuwa ni lazima litangazwe,kwa jinsi mchezo ulivyokwenda na alivyohojiwa aliamini kwamba njama hizo zilipangwa na mkewe Marietha ingawa hakutaka kulipa wazo hilo kipaumbele.
“Si mwingine ni Marietha najua,sijui kama nitamsamehe”
Deo aliongea kwa hasira,alikuwa ana kila sababu za kulipitisha wazo lake kwamba Marietha ndiye mkandarasi wa kila kitu kilichotokea,hakuelewa amfanye nini endapo Mungu akimsaidia akitoka kituo cha polisi.
“Lakini kwanini anifanyie hivi?”
Deo alizidi kujiuliza maswali yasiyokuwa na majibu kamili.
Wakati akiwa juu ya kiti ndani ya chumba maalumu cha mahojiano askari walikuwa nje wanamtizama kupitia kioo kikubwa,wanamjadili.
“Mambo yatakuwa mabaya sasa”
Askari mmoja aliyeitwa Santos Alexandra alimuongelesha mwezanke,uso wake ulijaa hofu mno.
“Ukiwa una maana gani?”
“Wewe hujui?Wewe hujui kuwa Amadour katuingiza kwenye matatizo”
“Matatizo kivipi?Embu acha uwoga”
“Sio uwoga”
“Kumbe nini?”
“Sasa unadhani akizungumza na Ladislaus itakuwaje?”
“Atazungumza naye vipi?”
“Kwani huku hafikagi?”
“Tangu lini Captain Ladislaus akafika huku?”
Chumba alichowekwa Deo Karekezi kilikuwa ni cha siri mno,hata mkuu wa kituo hakuelewa kwamba kuna mtuhumiwa wa madawa ya kulevya aliyeitwa Deo,kumaanisha kwamba hakuandikiwa faili.Uwepo wa Deo kituoni ulikuwa kimagendo!
“Wiki iliyopita alipita huku”
“Hawezi kupita,Ongea na Amadour afanye mambo chapchap”
“Sawa”
Askari waliendelea kubadilishana mawazo ni kitu gani wakifanye kwani walionekana kuingiwa na wasiwasi kupita kiasi,endapo mkuu wao wa kazi angejuwa mambo wanayoyafanya basi jela ingewahusu na wangelipa faini ya mabilioni ya pesa!

**** ******

Captain Ladislaus alikuwa ni raia wa Kifaransa lakini maisha yake yote alikulia nchini Sweden jijini Stockholm.Ingawa alisoma masomo ya biashara lakini siku moja alitamani kuja kuwa askari.Mwaka 1985 alimaliza kidato cha sita katika shule ya kiseminari katika jiji la Falun hapo hakutaka kuendelea tena kubaki nchini,akaenda kujiendeleza kimasomo nchini Afrika Kusini na baadaye akaenda kumalizia elimu ya ngazi za juu nchini Uingereza,huko ndipo alipobahatika kupata marafiki wengi wa mataifa mbalimbali.Ladislaus alikuwa kipenzi cha watu.Alivyorudi nchini kwake Ufaransa mwaka 1996 alianza kazi rasmi jijini Paris kama Sirgent,uchapakazi wake na uhodari kazini vikafanya apande cheo taratibu,miaka minne badaye akapewa cheo cha Captain,ilikuwa heshima kubwa sana katika familia yake.
Swala la ujambazi na rushwa vilipunguwa na hiyo ikamfanya apendwe na maskini na wanyonge ingawa alichukiwa na matajiri mbalimbali lakini hakujali.
Siku moja alivyokuwa ofisini kwake kuna kitu kilimsukuma atoke na kwenda kumimina kahawa mwenyewe.
“Captain,wacha nikakuchukulie kahawa,kapumzike”
Sauti hiyo ilitoka kwa askari aliyekuwa pembeni ameketi juu ya meza yake baada ya kumuona bosi wake anatembea kuelekea sehemu lilipo jiko.
“Hapana,wewe kaa tu.Nataka kunyoosha nyoosha miguu”
“Hapana kapumzike”
“Genzel,endelea na kazi”
Jiko na chumba alichokuwa amehifadhiwa Deo Karekezi vilikuwa karibu kabisa,Captain akaingia jikoni na kumimina kahawa.Lakini alivyokuwa nayo mkononi,alitaka kutembea na aone mazingira kwa niya kunyoosha miguu.Akatembea mpaka pembeni ya kioo kikubwa!Mwanaume aliyemuona amepigwa pingu amekalishwa ndani alimshtua kupita kiasi,isingewezekana hata kidogo kumkuta mahali kama hapo.Bila kujiuliza mara mbilimbili akafungua mlango na kuingia ndani,Deo alivyoinuwa macho yake hata yeye alionekana kustaajabu.
“Deooo”
Captain Ladislaus ndiye alikuwa wa kwanza kuita, hapo ndipo Deo alipogundua kuwa mtu aliyekuwa mbele yake,hakumfananisha.
“Ladislaus Navaro!”
Deo nayeye akaita kwa mshangao wa waziwazi.
“Mbona upo hapa Deo?”
Captain Ladislaus aliuliza kwa mshangazo na kusogea karibu zaidi,haikuwezekana kwa mtu mpole kama Deo kuwepo mahali kama hapo ingawa waliachana miaka mingi sana chuoni Uingereza mbali na hapo Ladislaus na Deo walikuwa ni marafiki wa karibu ingawa walichukuwa masomo tofauti.
Hapo ndipo Deo aliposhindwa kuvumilia alizungumza kwa uchungu sana na kusema kila kitu kilichotokea,Captain Ladislaus alisikitika sana na kuguswa mno.
“Subiri kidogo”
Hakuna siku aliyowasha kivumbi kama siku hiyo,Captain Ladislaus aliingia ofisini kwake akiwa amevimba kama chura,alikasirika kupita kiasi.Wote waliohusika na kitendo hiko waliwekwa nyuma ya nondo na Deo aliachiwa huru,akapewa kila kitu kilichokuwa chake!
**********
“Ng’aaaa ng’aaaa ng’aaaa ng’aaaaa”
Abraham alikuwa akilia kwa sauti lakini hakuwa ana msaada wowote ule,Mama yake alikuwa amelazwa juu ya kitanda anaingiliwa kimwili na Amadour,kifupi Marietha alikuwa mtumwa wa ngono wa Amadour na alifanya hivyo akiamini kwamba atamkomboa kutoka kwenye kitanzi kinachomkabili,Amadour alikuwa juu yake amemkandamiza anafanya naye ngono,moyoni aliumia lakini hakuwa na jinsi,ilikuwa ni asubuhi siku iliyofuata aliyoambiwa kwamba hiyo ndiyo ingekuwa siku ya mwisho ya Deo kunyongwa,ili kitanzi kimpitie pembeni ilikuwa ni lazima akubali kufanya naye tendo hilo baya la kuzini kwa mara ya mwisho,akiwa chini Amadour juu yake aliona mlango unafunguliwa.
Akakaza macho mlangoni,hakutaka kuamini mtu aliyemuona mbele yake.Alivyotaka kumtoa Amadour alishindwa,macho yake hayakumdanganya alikuwa ni mumewe Deo amesimama mlangoni,analia kwa uchungu machozi yanambubujika kama mtoto mdogo!Deo alihisi uchungu ajabu,bado hakutaka kuamini kama ni kweli mkewe anamsaliti na picha aliyoiona ilitosha kabisa kupata jibu lake kwamba Marietha alikuwa mkandarasi wa kila kitu kilichotokea!




Ukiachana na siku ambayo iliyokuwa chungu kwake alivyokuwa mtoto wa miaka kumi alivyomshuhudia Mama yake akipigwa mpaka kuzirai na Baba yake mzazi akidhani kwamba hatokuja kuumia kama siku hiyo habadani.Leo hii alimshuhudia mkewe yupo kitandani uchi wa mnyama amelazwa chali amepanuliwa miguu yake anafanya ngono na mwanaume mwingine,moyo ulimuuma hakuna mfano,ilikuwa ni kama mtu yupo ndani yake ameshika mtima wake akawa kama anauchoma na mishale ya moto,machozi yalianza kumbubujika na bado hakuelewa ni hasira ama wivu.Deo alikuwa bado amesimama pembeni ya mlango,pembeni chini alikuwa mtoto wake mdogo Abraham, analia kwa sauti kubwa.Alihisi kuishiwa nguvu mwili mzima,alitamani kutembea na kumvaa Amadour lakini hakuelewa nini kimetokea sababu mwili wake ulikuwa kama umepararaizi.Sio kwamba Marietha hakumuona Deo,alimuona na alidhani wenda anaota ndoto ingawa alitamani iwe hivyo alimuona vizuri sana Deo karibu na Mlango analia machozi,hata yeye alihisi kuishiwa nguvu,akajaribu kumsukumiza Amadour aliyekuwa juu yake anamla uroda lakini haikuwa kirahisi sababu hata yeye hakutaka kukatishwa starehe yake mbali na hapo hakuelewa kama mlango umefunguliwa na Deo yupo ndani tayari,kwa kuwa alikuwa anakaribia kufika mshindo haikuwa rahisi kung’oka juu ya kiuno cha Marietha,aliendelea kukinyonga kiuno chake huku akisema kwamba ‘MARIETHA YOU SO SEX AAH MAR..ETHA AAAAH BEBIII,ROLL IT,I LOVE YOU’hayo ndiyo maneno yaliyokuwa yanamtoka Amadour akiwa masikioni mwa Marietha,ni wazi kuwa alikuwa anakaribia kufika mlima kitonga.Alivyopasua yai la bata akalala na kutulia kifuani kwa Marietha,yote hayo yalishuhudiwa na Deo Karekezi,alikuwa akimwaga machozi kama mtoto mdogo, mapigo yake yalikuwa yakidunda kwa nguvu kama kitenesi,hiyo ilimpelekea mapafu yake yajae hewa,kifua chake kikaanza kupanda juu na kushuka chini.Bado hakutaka kuamini.
“Marietha, I love you.Please leave Deo and stay with me”(Marietha,nakupenda.Tafadhali achana na Deo baki na mimi)
Hayo ndiyo yalikuwa maneno ya kimahaba kutoka kwa Amadour akiwa kifuani kwa Marietha.Sijui nini kilimwambia ageuze shingo yake nyuma,moyo wake ulishtuka kupita kiasi baada ya kumshuhudia Deo pembeni ya Mlango anawatizama,kama chui akaruka upande wa pili.Amadour alikuwa mkorofi lakini siku hiyo alijishangaa kwanini anaogopa,moyo ulimwenda mbio bado hakutaka kukubaliana na macho yake kwamba mtu aliyekuwa mbele yake yupo huru,haikuwezekana hata kidogo kuamini kwamba Deo ameachiliwa bila yeye.
“Endele..ni tu”
Deo aliongea lakini kwa kujikaza,alijitahidi kuvumulia lakini sio siri machozi yalikuwa yanambubujika kama mtoto mdogo vile.Ulikuwa ni usaliti wa hali ya juu na hakuelewa amfanye nini mkewe aliyekuwa kitandani,akiamini kwamba ndiye amemuwekea madawa ya kulevya ili anyongwe.Hakutaka kubaki ndani ya chumba hicho,alichofanya ni kutembea mpaka kwa mtoto wake Abraham aliyekuwa chini analia,akamnyanyua na kumuweka mikononi mwake kisha kutoka naye nje.

Kama siku hiyo Marietha angepimwa akili zake na majibu yangetoka angepelekwa moja kwa moja milembe sababu alikuwa kama mwendawazimu ama mwehu,hakuelewa ni kitu gani akifanye.Alishaelewa ndoa yake ilikuwa tayari imevunjika na hilo lilikuwa wazi kabisa,lilikuwa ni fumanizi la ana kwa ana,Deo alikuwa ni mwanaume mwenye hasira kupita mbogo na mpaka dakika hiyo hakuelewa ni kwanini ajamvaa na kumpiga makofi badala yake alimchukuwa Abraham na kutoka nje.Bado alikuwa yupo kitandani,alihisi mwili wake kama umepigwa shoti ya umeme!
“Yule ni Deo?”
Lilikuwa ni swali la kipumbavu na lenye mauzi na Amadour ndiye aliyeuliza hata yeye bado hakuwa ana uhakika wenda ndiyo maana akauliza sababu alijuwa kwa wakati huo Deo alikuwa ndani ameshikiliwa kituoni,hiyo ilimfanya ajitutumue na kupeleka mkono chini akanyanyua suruali yake ambapo alitoa simu yake na kuwatafuta askari aliochonga nao dili mpaka Deo akatupwa ndani!
Majibu ya maaskari yalimvuruga akili yake kwa kiasi cha kutosha!
“Unasemaje wewe?”
“Nasema kwamba,Unatafutwa. Amadour umenitia kwenye matatizo makubwa sana.Sasa hivi sina kazi na nimeshtakiwa kwa upuuzi wako,najuta sana”
“Sikuelewi,embu nyoosha maelezo.Kwanini Deo yupo huru?Ana pesa gani mpaka awe nje?Mimi nimewalipa hela tukakubaliana kwamba atoke mpaka nitakapomaliza shughuli zangu,kwanini iwe hivi?”
Amadour alifoka simuni lakini alionekana mwenye mashaka sana!
“Nasema hivi,unatafutwa na jeshi la polisi ndugu yangu.Ndiyo nataka kukupasha”
“Kwanini?Kivipi?”
“Kivipi nini?Amadour,kifupi umeniponza sitaki tena mazungumzo nawewe”
“Hiv…tititi”
Hapohapo simu ilikatwa.
Hiyo ilimfanya aogope na ujanja wake wote ukawa mfukoni.
“Marietha usiwe na wasiwasi mambo yote yatakuwa bomba,nakuja sasa hivi”
Amadour alizungumza akijifanya haogopi kitu chochote kile.Marietha hakujibu chochote alikuwa ameganda analia machozi, anatafakari amwambie kitu gani Deo amuelewe,kwake ilikuwa ni ngumu kumeza.
“Naondoka lakini nitarudi”
Amadour alizungumza huku akiwa anavaa suruali yake ili atoke haraka sana eneo hilo.Kila kitu kilivyokuwa sawa alifungua mlango na kutoka zake,kitu kilichomkuta nje alikiogopa.
Alikumbana na lundo la maaskari nane nje ya lango la Hotel,akajifanya awaoni na kuwapita.
“Excuse me,Excuse me”
Askari mmoja alimsemesha akiwa nyuma yake lakini yeye akajifanya mkaidi,akazidi kusonga mbele.Hapo ndipo askari hao walipoanza kumfuata kwa nyuma na kumshika bega.
“Nadhani wewe ni Amadour Estemole”
Askari mmoja aliyechomekea amevalia sare za kipolisi bastola kiuoni, alimuuliza Amadour.
“Ndio mimi nikusaidie nini?”
“Naomba tuongozane nyumbani kwako,tunahitaji kusachi”
“Kwanini?Embu njooni tubonge huku mara moja”
Amadour alielewa kila kitu kitachoenda kutokea na niya yake ilikuwa kuwapeleka maaskari faragha ili awape kitu kidogo cha kuwafunga midomo ili wasimgasi lakini hiyo haikuwezekana sababu walipewa amri kutoka ngazi za juu.
“Askari dola elfu moja ninayo hapa ya chai na soseji,mengine tutazungumza, sawa?”
“Hapana twende nyumbani kwako”
Askari walikomaa mwanzo mwisho na hatimaye Amadour akawekwa chini ya ulinzi mkali na kuingizwa ndani ya gofu la polisi,safari ya kwenda nyumbani kwake mtaa wa Alasta morka kuanza mara moja.Na walivyotia maguu cha kwanza walipekua geto la Amadour chumba kwa chumba,walikumbana na silaha za moto pamoja na paketi mbili za madawa ya kulevya aina ya Herroin mbali na hapo walikuta vifurushi vya bangi chini ya godoro lake,wakazidi kufukunyua zaidi.
“Hii passpot kumbe unayo wewe?Hii passpot ya Deo Karekezi inafuata nini hapa nyumbani kwako?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Captain Ladislaus Navaro,tena akiwa na jazba kupita kiasi chake.
“Nakuuliza swali nahitaji jibu mara moja”
“Hii passport itakuwa aliisahau hapa nyumbani kwangu na isi…”
Amadour alinyamazishwa na kibao kikali cha uso kutoka kwa Captain Ladislaus Navaro, majibu aliyoyasikia yalikuwa yakimchefua mno na katika yote alishajuwa kwamba Amadour ndiye mkandarasi wa kila kitu kilichotokea!Kulikuwa hakuna cha msalia mtume,Amadour akapigwa pingu na kubebeshwa vitu vyake vya magendo viwe kama vithibitisho,moja kwa moja akaingizwa ndani ya gari na safari ya kwenda kituoni ikaanza dakika hiyohiyo.Deo aliitwa kituoni na kupewa Passport yake,hakuonesha kuwa na furaha yoyote ile uchangamfu wake wote ulichukuliwa na fumanizi la mkewe chumbani.
********
Ukweli ulibaki kwamba Marietha na Amadour ndiyo walifanya mpaka yeye atake kufungwa gerezani na baadaye anyongwe,hivyo ndivyo Deo aliamini.
Kifupi alijutia kuingia jijini Paris alimchukia Marietha kiujumla na hakuelewa amfanye nini lakini alimuomba Mungu sana amuepushe na hasira mbaya alizokuwa nazo.Hakurudi tena katika hotel aliyopanga,aliogopa kupata kesi ya kuuwa sababu alielewa ndicho kitakachotokea mbeleni,alitaka kujiepusha na hilo.Ndiyo maana akamchukuwa mwanaye na kukaa mbali na Marietha.Usiku mzima Abraham alilia akitaka kunyonya lakini Deo hakuwa na jinsi zaidi ya kutoka na kuelekea ‘supermaket’ huko alitafuta maziwa ya watoto, akanunua na kichupa kidogo!Akarudi hotelini na kumpa Abraham maziwa ya kopo,bado moyo ulimuuma mno.Usiku ulipita kukachuka,akamuweka mtoto begani na kuelekea moja kwa moja uwanja wa ndege Paris, Airport-Le Bourget!
Niya yake ilikuwa ni kubadili tiketi ili arejee nchini Tanzania japokuwa viza yake ilikuwa bado haijaisha wakati wake,alikuwa bado ana miezi mingine miwili ya kubaki nchini lakini hakutaka kujali hilo,mambo yaliyotokea yalimfanya atake kurudi mara moja iwezekanavyo.
“Ndio nataka kubadili tiketi dada angu”
Deo alikuwa mezani ofisini kwa msichana mdogo wa makamo wa kifaransa,begani yupo mwanaye Abraham.
“Kwahiyo unataka kuondoka lini?”
“Hata leo”
“Sawa subiri niangalie hapa kwenye mtandao kama kuna nafasi”
Msichana wa kifaransa mwenye nywele za singasinga aliigeukia kompyuta yake na kuanza kubonyeza ‘keyboard’
“Nafasi hapa ipo lakini saa sita ya usiku,Unabadilisha tiketi yako peke yako?”
“Ndio”
“Kweli?”
“Hapana na mwanangu huyu Abraham”
“Sawa subiri”
Mpango ukaanza mara moja wa kubadili tiketi,kuna kitu Msichana huyu aliyekuwa makini aligundua kwamba mteja aliyekuwepo mbele yake hakuja mwenyewe nchini Ufaransa.
“Lakini mlikuja watatu”
“Ndio”
“Huyu mwingine anaitwa Marietha Karekezi,ni mkeo?”
“Dada nikatie tiketi.Maswala mengine niachie mimi mwenyewe”
Deo aliropoka,hakutaka maswali mengine zaidi sababu yalikuwa kama yanamtonesha vidonda.
“Unaondoka na huyu mtoto?”
“Ndio,nilishakwambia”
“Bado ni mdogo sana”
“Nipe tiketi”
“Hapana siwezi kukupa.Sitoweza mtoto bado ananyonya”
Sekunde tano zilikuwa nyingi ukaibuka mzozo mkubwa,Deo aliwaka dada wa kifaransa nayeye akachachamaa akidai kwamba haitowezekana hata kidogo na walitumia lugha ya kiingereza.
“Nipe namba za tajiri yako”
“Hizi hapa,mpigie wala siogopi.Tena tumia simu yangu”
Hicho ndicho kitu kilichotokea Deo hakutania,akachukuwa simu na kumuibukia meneja wa kampuni ya ndege ya British Airways hewani na kumchana kila kilichotokea.
“Naomba nizungumze na huyo dada,samahani kwa usumbufu Mr.Deo”
Upande wa pili wa simu ulisikika kutoka kwa meneja aliyeitwa Von Rudolf,simu akapewa msichana wa kifaransa.
“Halloo Bosi,habari za asubuhi?”
“Nini kimetokea Chloe?”Akauliza kwa ukali kidogo.
Kila kitu kikawekwa wazi na mambo yalivyotokea,Chloe akazungumza kila kitu.
“Embu subiri kidogo”
Mr Von Rudolf alikuwa nchini Uingereza huyo ndiye alikuwa meneja wa kampuni ya shirika la ndege ya british airways nayeye akaingia kwenye mitambo ya kompyuta.Ni kweli Deo hakustahili kusafiri na Abraham.Alichofanya Von Rudolf ni kuingia moja kwa moja kwenye ‘system’ kuna kitu alikigundua lakini kwa juu juu,habari za Deo zilikuwepo na alipewa taarifa na Uongozi wa Ufaransa.Akarudi kwenye laini.
“Chloe”
“Abee”
“Hakikisha anasafiri na mkewe”
“Sawa bosi”
Chloe alikata simu akamwambia Deo kila kitu kilivyoenda.Hata iweje ilikuwa ni lazima arejee nchini Tanzania.
“Sawa badili zote”
Tiketi ya Marietha ikabadilishwa na ilitakiwa usiku wa siku hiyo waondoke na shirika la ndege ya Turkish Airways ambapo asubuhi yake wangeunga na Bristish airways wakiwa nchini Uingereza.
Mambo yakawekwa vizuri tiketi tatu zikawa tayari.
“Ahsante nashukuru”
“Karibu tena”
Deo akasimama na kuondoka!
*********
Usiku mzima alikesha kwa kulia mpaka machozi yakamkauka,bado hakuelewa ni kitu gani akifanye.Alimlaumu shetani kwa kumuingiza katika majaribu akaisaliti ndoa yake na kuzini na Amadour, ingawa alikuwa mwenye msimamo lakini hakuelewa hata yeye ilikuwaje akapanua miguu yake na kumruhusu Amadour auone uke wake!
“Lakini nilifanya hivyo kwa ajili ya Deo”
Aliwaza Marietha na kuzidi kutafakari,moyo ulimuuma kwa kiasi cha kutosha.Alimsubiri Deo usiku mzima lakini hakukuwa na dalili yoyote ile hisia zake zilimtuma kwamba Deo amesharejea tayari nchini Tanzania, mpaka inafika saa kumi za asubuhi Deo hakuonekana.Wazo lililomjia kwa wakati huo ni kutokomea lakini hakuelewa ni wapi aende,akaweka vitu vyake sawa ndani ya begi na kutoka nje,ni wazi kuwa alikuwa mgeni wa jiji lakini hilo hakujali.Akatoka mpaka mapokezi na kuanza safari ya kutembea!
*********
Deo alizama ndani ya hotel aliyofikia na kuingia mpaka chumbani baada ya kutoka kubadili utaratibu wa safari,tiketi alikuwa nazo mkononi niya yake ilikuwa ni kumkabidhi Marietha ili waondoke siku hiyohiyo lakini Mkewe hakuwepo,akatizama huku na kule lakini wapi,akaingia bafuni lakini hakukuwa na dalili yoyote ile.Alivyoingia kabatini hakukuta nguo za Marietha wala begi,hapo ndipo taa nyekundu ilipoanza kuwaka kichwani kwake kwamba ni kweli Marietha na Amadour ni wapenzi na tayari amekimbiwa,roho ilizidi kumuuma hakuna mfano wake!Alichofanya ni kuweka nguo zake ndani ya begi tayari kwa safari ya usiku huo kurudi nchini Tanzania akiwa na mwanaye Abraham.



Deo alikuwa mwenye mawazo chungu mzima ndani ya kichwa chake, furaha aliyokuwa nayo akiamini kwamba ataenda kuimalizia nchini Ufaransa na mkewe sasa iligeuka na kuwa chungu kama shubili.Na alihisi kuna kitu kimepungua ndani ya mwili wake mbali na hapo moyo wake uliendelea kumuuma kwa kiasi cha kutosha, bado picha ya Marietha akiwa juu ya kitanda anafanya ngono na Amadour ilimsumbua sana,ni wazi kwamba katika maisha yake alishuhudia matukio mengi yaliyomuumiza mtima lakini hilo lilizidi kipimo chake,hakuweza kulifananisha na lingine lolote lile sababu alilichukulia ni dharau na alimuhukumu moja kwa moja Marietha kwamba alitaka kumuuwa,alikumbuka mapendo yote aliyomuonesha hapo ndipo alizidi kuumia zaidi na zaidi.Taratibu alianza kupanga nguo zake ndani ya begi,hakuelewa atawajibu nini ndugu zake ama marafiki zake endapo watamuuliza yu wapi Marietha?Aliamini angeumia zaidi na kutoneshwa vidonda.
“Ng’aaa ng’aaaaaa”
Sauti ya Abraham ndiyo iliyomuibua kutoka katika dimbwi la mawazo,hakuwa na kitu kingine zaidi ya kumbembeleza mwanaye sababu aliamini huyo ndiye faraja yake kwa wakati huo.
“Shiii shiii shiiii shiiii shiiiii,nyamaza mwanangu usilie..Shiii shiiii shiiii”
Kibarua cha kumtuliza mwanaye asipige kelele kilianza,alifanya hivyo na kutoa kikopo cha maziwa kisha kumpa,hatimaye Abraham akanyamaza!Hilo lilivyoisha akaendelea kupanga nguo moja baada ya moja ndani ya begi na kila kitu kilivyokaa sawa,akatupa tiketi ya Marietha juu ya kitanda na kuanza safari ya kuondoka zake kutoka nje ya hoteli ili atafute usafiri mpaka uwanja wa ndege akasubiri ndege ya Usiku atokomee na kurejea nchini Tanzania.
Aliamini safari nzima kwake itakuwa chungu kuliko kitu chochote kile na ingekuwa tofauti kabisa ama alivyokuwa anasafiri na mkewe mpaka nchini Ufaransa akiwa mwenye furaha tele!Aliamini kwamba safari ya Ufaransa ndiyo iliharibu furaha katika maisha yake,kifupi aliichukia kuanzia siku hiyo na aliapia kwamba hatokuja kukanyaga tena.Mtoto mchanga begani kwake,mkononi akiwa ana buruza begi lake akaanza kutoka nje taratibu,akaingia ndani ya lift na kubonyeza herufi ‘G’ kumaanisha impeleke mpaka chini kabisa kutoka gorofa namba nane,ilivyomfikisha mpaka chini ikatoa kimlio kumaanisha kuwa imefika,mlango ukajifungua akaanza kutembea kutoka nje.
“Taxiiii,Taxiiiii”
Deo aliita kwa sauti baada ya kuona gari ya njano na juu ina kibao kilichoandikwa ‘TAX’,gari ikasogea mpaka miguuni mwake.
“Take me to Airport-Le Bourget”
Deo alitaka apelekwe uwanja wa ndege dakika hiyohiyo.
“Get in my friend”(Ingia ndani rafiki yangu)
Deo na mizigo yake pamoja na mwanaye kipenzi wakaingia ndani ya taxi.
“Let’s go,What are you waiting for?”(Tuondoke,unasubiri nini)
Deo akauliza sababu dereva wa taxi alikuwa bado hajaondosha gari na macho yake yalikuwa juu ya kioo cha katikati, ilielekea kuna kitu alikiona ndio maana alisita kuondosha gari,ni kweli alimuona mwanamke mmoja yupo nyuma ya gari umbali wa mita kama kumi hivi anapunga mkono huku anakimbilia taxi.Jambo hilo lilimshangaza sana dereva, hakuelewa kwanini mwanamke huyo anakimbia kiasi hiko,alijuwa fika kuwa anamkimbilia yeye lakini bado hakumjua akili yake ikamtuma wenda alikuwa mmoja wa abiria wake na alisahau kitu.
“Deoooooo”
Maskini ya Mungu alikuwa ni Marietha,anahema juu juu na alifika upande wa Deo na kumuita.Sio kwamba Deo hakusikia anaitwa.
“Drive”
Kauli hiyo ilitoka kwa Deo bila kumuangalia Marietha usoni aliyekuwa nje ya gari.Dereva alivyotaka kuliondosha gari moyo wake ukasita.
“Why are you hesitating?”(Mbona unasuwa)
Deo akafoka kwa sauti akimkaripia dereva.
“Deo mume wangu naomba uni…”
Deo hakutaka kumuangalia Marietha machoni,alihisi kichefu chefu cha kutapika na hasira kupita kiasi ndiyo maana alimsisitiza dereva aondoshe gari mara moja tena bila kupoteza muda,hiyo ilimfanya Marietha amwage machozi na kusema kwamba anahitaji walau dakika moja ajielezee lakini hiyo haikusaidia,Deo alikula buyu na hakutaka kujibu zaidi tu alimwambia dereva atoe gari!
Kwa kuwa mteja mfalme siku zote na alitaka pesa dereva alipiga gia na kuanza kutoa gari.Kama swala Marietha akaruka kwa mbele.
“Nigonge tu D..eo nata..ka ku..fa De..o nakupenda mum..e wangu ni..pe dak..kika moja tu.Naomba unisikilize”
Lilikuwa ni jambo la kushangaza ambalo halikuwahi kutokea nchini Ufaransa,wakazi wa jiji hilo waliacha shughuli zao na kumshangaa Marietha aliyekuwa amepiga magoti mbele ya gari analia machozi anazungumza lugha ambayo hawaielewi.Watu wengine walidhani wenda mwanamke huyo yupo katika maigizo na pembeni ama mbali kuna kamera inamrekodi ili watoe sinema lakini haikuwa hivyo kwani Marietha alikuwa akiililia ndoa yake ambayo tayari iliingia doa.
“Sir i can’t drive”(Mzee siwezi kuendesha)
Dereva aliingiwa na huruma na alikataa kutoa gari,hiyo haikumfanya Deo abadili maamuzi yake.Hakujibu chochote bali alitoa mizigo yake ndani ya gari na kumuweka mwanaye begani vizuri,akaanza kutafuta usafiri mwingine.Ni wazi kwamba moyo wake haukutaka kumuona mwanamke aliyeitwa Marietha mbele ya macho yake.
“De..o naomba nip..e se..kund..e moja nizu..ngumze nawewe tafadhali”
Marietha alikuwa akilia kwa kwikwi huku akitembea kwa magoti ilikuwa ni picha ya kuuzunisha kupita kiasi chake sababu alikuwa akilia mbele ya umati wa watu na wala hakuogopa alichojali yeye ni ndoa yake na si vinginevyo,akatembea kwa magoti na kuikamata miguu ya Deo.
“De..o ni sam..ehe mume wa..ngu”Alisema Marietha!
Tukio hilo lilijaza watu na kila mtu alikuwa akimshangaa Marietha na baadhi yao wakadiriki kuinua simu zao na kuanza kuchukuwa video.
“Marietha niache”
Deo akajibu kwa hasira na kujaribu kurusha mguu lakini hakufanikiwa sababu Marietha alimkamata huku akimwaga machozi na kutoa kamasi,ni wazi alihitaji msamahaa sababu aliamini alifanya hivyo kwa ajili ya Deo asiuwawe sababu anampenda lakini badala yake alichukuliwa msaliti na Malaya mchafu!
“De..o si..wezi kuku..acha nakupenda mume wangu”
“Acha unafki,niachie nimekwambia”
“Siwezi Deo”
“Marietha niachiee”
“Si..wezi.Deo usiniache tafadhali”
“Marietha niachie”
“Ha..pana mume wangu”
Kuiachia miguu ya Deo ilishindikana na alielewa kwa kitendo cha kufanya hivyo angeachwa,Marietha aliendelea kulia huku akiwa ameishika miguu ya Deo akimwambia kwamba ampe walau sekunde moja aseme kilichotokea lakini haikuwezekana kwani Deo alimvuta na kumsukuma kando, Marietha akadondoka chali juu ya barabara ya lami,jambo hilo liliwashangaza sana wazungu na walimuona Deo ni mnyanyasaji wa kijinsia sababu katika nchi ya kifaransa wanawake walipewa kipaumbele kuliko kitu chochote kile.
“Deoooo.De…..o”
Marietha aliita huku akibubujikwa na Machozi akimshuhudia Deo anaingia ndani ya gari jingine na kuondoka zake,sio siri hakuelewa ni kitu gani akifanye moyo wake ulimuuma ajabu na hapohapo shetani akamvaa na akamsukuma kwenda kumeza sumu na kujiua sababu alijua bila Deo maisha si chochote na alivyokumbuka unyama aliofanyiwa na Amadour aliumia moyo zaidi
******* *******
Picha ya mkewe akiwa amepanuliwa miguu yake anafanya ngono na Amadour bado ilimsumbua kichwani,hakustahili kufanyiwa unyama kama huo tena nchi za watu.Na hiyo ilimpelekea mpaka kuwaza na kujuta kwanini alimuoa Marietha,kifupi alijisikia uchungu na ilimpelekea amwage machozi yakamchuluzika mpaka kwenye mashavu na kudondoka juu ya shati lake,dereva aliyemkodi alikuwa mbele akavuta kioo cha katikati ili kumwangalia abiria wake.Deo alikuwa akilia machozi na alikuwa akimlilia mkewe, ghafla picha yake akiwa ndani ya suti kanisani ikamjia na akaanza kukumbuka matukio yote aliyomfanyia kwa nguvu ya penzi akaamua kuja naye nchini ufaransa ili amfurahishe lakini matokeo yake alisalitiwa vibaya sana.
“Marieth….a”
Deo aliropoka na kumfanya dereva Taxi ageuze shingo yake nyuma.
“Are you talking to me?”(Unazungumza na mimi)
Dereva akauliza sababu alijua wenda anaongeleshwa.Hiyo ndiyo ilimfanya Deo alie zaidi,machozi ya uchungu yalimtoka akawa anavuta kamasi mbali na hapo hakujuwa kwanini analia.
“Boss,any problem?”(Tajiri,tatizo lolote)
Dereva akauliza tena ili kumdadisi lakini Deo hakuwa tayari kufungua kinywa chake na kuzungumza aibu aliyopata.
“Ju..st dri.....ve the car”
Deo alizungumza kwa kwikwi akimwambia dereva aendelee na safari kumaanisha kwamba hakuwa tayari kuzungumza jambo linalomsibu,dereva akabadili gia na kuongeza mwendo!
**********

Alikuwa ni kijana wa kipare mweusi na mrefu,amejazia mwili na ungeuona mwili wake ungeweza kusema kwamba ‘Hili lijamaa linakula kokoto’mkono wake ulijazia misuli na kifua kilifanana na mcheza mieleka nchini Marekani,John Cena!
Koba badala ya kuutumia mwili wake vizuri yeye aliutumia kufanya ubabe na kupora mali za watu,baada ya kuiba sana Arusha na kuvamia benki,mapolisi walikuwa wanamtafuta kwa wudi na uvumba sababu ya kifo cha mfanyabiashara mkubwa George Mshana mbali na hapo alishawahi kuvamia kituo cha polisi cha Njiro na kuuwa askari tisa.Kifo cha maaskari ndicho kilichoinua chuki kubwa dhidi yake hapo ndipo walipoamua kula sahani moja na jambazi Sugu Koba ingawa hawakufanikiwa sababu aliwazidi akili.
Koba aliamua kukimbilia jijini Dar es salaam mwaka 1997 akatokomea jijini Dar es salaam kwa lengo la kujificha huko akabadili jina na kujiita ‘Scorpion’mpaka hapo akawa amefanikiwa kunyuti mitaa ya Buguruni sokoni!Siku zote tabia ni kama ngozi, hakuweza kubadilika kamwe akaanza kuiba taratibu na wakati mwingine aliuwa watu kwa kuwatoboa macho yao.
“Kelele wewe toa pesa,tuliaaa”
Koba ama Scorpion alikuwa kamkaba mtu lengo lake lilikuwa ni kumuibia kama anavyofanya siku zote na mkononi alikuwa ameshika kisu kikali chenye makali kotekote.
“Kaka sina pesa si si sina kweli tena”
“Mimi sio kaka yako,toa pesa”
“Sina sina”
“Una nini?”
“Nina jero tu hii hapa tena”
“Unaleta utani sio?Dharau eeeh?”
“Kweli”
“Kwanini hutembei na pesa?Ukiumwa je?Utaendaje hospitali?”
“Nikiumwa basi, ndugu zangu watanipeleka hospitali”
“Ukiumwa basi,sasa ngoja nikuoneshe”
Scorpion bila huruma yoyote akainua kisu na kutumbukiza machoni kwa kijana huyo mdogo baada ya hapo akamchoma visu vingine vya tumbo,akamburuza na kwenda kumtupa barabarani kisha kutokomea pasipo julikana.
Lilikuwa ni tukio kubwa na lililowagusa watu,kila mkazi wa Buguruni alimwaga machozi na jiji zima la Dar es saalam kwa ujumla.Kifupi tukio hilo lilitingisha jiji zima,baada ya kuchunguza vizuri na kufanya msako wakapata fununu kwamba mtu huyo anaitwa Koba na alikuwa muhalifu mkoani Arusha.Siku iliyofuata hakuna askari aliyelala ni simu ndizo zilizokuwa zinaruka,askari wa Arusha wakajuwa mtu wao yupo jijini Dar es salaam.Kwa usongo waliokuwa nao wakatuma maaskari chini kwa chini.
*********
Scorpion aliendelea kuliza watu na kuendelea kuibia raia na kuwauwa kila ikifika usiku,siku hiyo usiku ilinyesha mvua kubwa kupita kiasi na alijisikia kuiba pesa nyingi sana.
“Leo naenda kuiba sheli”
Scorpion aliwaza na kuchomoa bastola chini ya godoro,akakagua kama ina risasi na kuiweka kibindoni.Akasubiri mpaka giza liingie ndipo akatoka nje,mvua ilimlowesha lakini hakujali,alitembea mpaka sehemu zilipoegeshwa taxi nyingi na kuchaguwa moja wapo nzuri na mpya.
“Mambo vipi jombaaa?”
Scorpion alitoa salamu kwa dereva taxi.
“Poa”
“Nipeleke Tegeta”
“Tegeta sehemu gani?Alafu ingia ndani unanyeshewa hapo broo”
Dereva taxi alijifanya mkarimu,hakuelewa kwamba huruma yake inamuingiza kwenye matatizo makubwa mno.Scorpion akazama ndani ya gari na safari ikaanza dakika hiyohiyo.
“Washa gari Mwita,Washa gari”
“Una uhakika ameingia humo?”
“Ndio,washa gari”
Kumbe tangu Scorpion anatoka nyumbani kwake maaskari walikuwa nyuma yake wanamuangalia kila anapokwenda na alivyoingia ndani ya taxi walimuona, hapo ndipo nao wakawasha difenda zao tayari kwa ambush!
“Kacha kacha”
Mwita alikoki bastola yake huku mtutu wake ukiwa begani kwa lolote lile.
Scorpion alikuwa ndani ya taxi anazungumza na akili yake jinsi atakavyovamia ‘patrol station’ na kuiba pesa kisha atokomee na gari.
“Tegeta sehemu gani broo?”
Dereva tax akauliza.
“Afrikana”
“Poa”
Taxi ilisonga mbele na walivyokaribia kufika Afrikana Scorpion akatoa simu na kuzuga anazungumza na mtu.
“Wapi upo?Hapo sheli eee?Basi poapoa”
Alivyokata simu alitoa amri na kusema kuwa ashushwe sheli ya mafuta,dereva hakuwa na tatizo.Akapiga kona kitendo cha dereva kuweka mguu kati Scorpion aliachia risasi mbili hewani.
“Paaaa paaaaaa”
Watu wakaanza kusambaa huku na kule lakini kabla ya kushuka na kufanya lolote zilisikika risasi nyingine kutoka nyuma,askari walikuwa tayari wamefika na kitendo cha kusikia milio ya risasi kiliwafanya na wao wafumuwe ili kujihami.
“Paaa paaa paaaaa”
Scorpion nayeye akaanza kuwarushia risasi lakini alizidiwa sababu askari walikuwa wengi.
“Endesha gari fasta”
Zoezi likabadilika hapohapo,bastola ikawa kichwani kwa dereva taxi hiyo ilimfanya mpaka amwage mkojo maana roho yake ilikuwa mkononi.
“Endesha gari fasta nimesema”
Dereva akapiga gia na kusonga mbele,mvua ilikuwa kubwa kupita kiasi hiyo ilifanya barabara iwe na utelezi mno.
Kwa kuhofia kifo dereva akazidi kusonga mbele zaidi akaivuka Tegeta nyuki na kuzidi kuendelea na safari,alijuta mno kwa kubeba jambazi na hakuelewa siku hiyo mwisho ungekuwa ni kitu gani,alipandisha gia na kufika msitu wa madare hapo ndipo akili ilipomjia,aliona kimlima kidogo ambacho kina msitu,akazidi kuongeza mwendo zaidi akaangalia vizuri kama amefunga mkanda wa kiti,bila kujifikiria alilipeleka gari kwenye korongo la mlima niya yake ilikuwa ni kulipindua ili ajinusuru na kifo mbeleni ingawa hakujuwa kama atapona,likabiringika mara tatu na kugota kwenye mti.
Kutokana na Scorpion kutofunga mkanda ilifanya atoke nje ya kioo na kudondokea upande wa pili.
Askari na wao wakapiga msele na kabla ya gari lao halijasimama walitua ardhini kama makomandoo vitani,waliingia msituni na kuanza kumsaka jambazi Scorpin.
“Yule pale…Paaa paaaaa”
Askari walirusha risasi walivyomuona Scorpion anakimbia.
*******
Mbele yake hakujua kitu kingine zaidi ya kifo tu,maji yalikuwa mengi na tayari yalimzidi kimo sababu ya mvua kubwa kunyesha bila kukoma,ulikuwa ni usiku mkubwa na kabla ya kukata roho aliamua kusali sala yake ya mwisho na kumuomba Mungu amnusuru na kifo kibaya anachoenda kupambana nacho shimoni.Issa alikaa masaa mengi shimoni akiwa ana njaa, nguvu zilimuishia sababu ya njaa, hiyo ilimfanya ashindwe kupiga mbizi.Lakini kwa mbali alisikia milio ya risasi lakini hakuwa ana uwezo wa kufanya chochote sababu alijuwa kifo ni halali yake,alishakata tamaa ya maisha na kumuomba Mungu ampokee ahela!
**********
Scorpion alikimbia mbio za swala lakini aliteleza na kuanza kubiringika kama mpira, ghafla akakumbana na shimo akatumbukia,askari na wao walimfuata nyuma na kusimama nje, juu ya shimo.
“Ametumbukia humu”
Akasema askari mmoja.
“Tumtoe”


Haikuwezekana hata kidogo kwa askari kurudi kituoni mikono mitupu bila ya jambazi Sugu Scorpion,kwa kufanya hivyo waliamini kwamba wangesifiwa na pengine kupandishwa vyeo.Na kumkosa na kurudi kapa hiyo ingewapunguzia heshima kwenye kazi zao za kipolisi ingawa mvua ilikuwa kubwa na inawanyeshea lakini hawakutaka kubanduka, kwao kunyeshewa haikuwa kitu kabisa.Hivyo mitutu yao ilikuwa mikononi kwa lolote litakalo tokea.
“Afande kalete chepeo”
Kauli hiyo ilitoka kwa askari mmoja aliyekuwa kandokando na karibu kabisa ya shimo.Maji mengi yalikuwa yakiingia na udongo, ilikuwa ni lazima wachimbue na kumtoa Scorpion akiwa hai au mfu!Chepeo likaletwa, dakika hiyohiyo maaskari wakaingia mzigoni na kuanza kusambaratisha udongo uliokuwa unaingia ndani ya shimo kwa njia ya kuchota kifusi cha mchanga na kumwaga kando,ni wazi kwamba walichoka lakini hawakutaka kupumzika na walifanya zoezi hilo kwa staili ya kupokezana, akitoka huyu anamkabidhi yule mpaka wakafanikiwa kuona mkono wa mtu,kibarua kikaendelea mwishowe wakaona mwili wa mtu na kuutoa pembeni.
“Tayari tuondokeni”
Baada ya mwili kuwekwa pembeni askari mmoja aliyeonekana kuchoshwa na kazi hiyo alishauri.
“Embu subiri”
“Nini bwana”
“Huyu sio mwenyewe”
“Ukiwa una maana gani?”
“Nikiwa nina maana kwamba huyu sio jambazi tunayemtafuta”
“Embu tuondokeni afande,huoni tunazidi kulowana tumpakie huyo jambazi ndani ya gari tukam-minye mbele ya safari.Si amejifanya kafa atafufuka tu”
Kuzozana kwa maaskari kulimfanya afande Jumbo achukulie ni upotevu wa muda isitoshe alikuwa hoi bin taaban.
“Nasema kwamba huyu jambazi sio mwenyewe.Subiri muone”
Bila uoga afande mmoja wapo aliyekuwa ana roho ngumu alichuchumaa na kuugeuza mwili uliokuwa chini,kila mtu aliogopa mwanaume aliyekuwa amelala alikuwa amevimba kupita kiasi na isitoshe sura ilikuwa tofauti na jambazi Scorpion waliyekuwa wanamsaka kwa wudi na uvumba.Ilibidi waingie tena shimoni na kuanza kulifukua, hapo ndipo walipobahatika kumkuta Scorpion akiwa amefunikwa na matope,hawakuwa na muda wa kupoteza wakasaidiana na kumtoa nje kwa tahadhari sababu ya shimo lilikuwa linatitia hiyo ilifanya mpaka watumie kamba kuvutana,sio siri ilikuwa ni kazi ngumu mno Polisi wote walikuwa hoi baada ya kumtia Scorpion mikononi mwao.
“Na huyu ni nani?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Afande aliyefahamika kwa jina la Tumbo,ambalo halikuwa na jibu la harakaharaka sababu hakuna hata mmoja wapo kati yao aliyekuwa anajuwa sababu walikwenda pamoja.Hiyo ilifanya maaskari wote wakae kimnya.
“Huyu inabidi tumchukuwe keshakufa huyu,mpakie kwenye Diffenda tumpeleke Monchwari”
“Sasa hapimwi?”
“Apimwe nini?Nimesema twende awekwe ndani ya diffenda”
Mwili wa Issa ukabebwa na kupelekwa ndani ya Diffenda na safari ya kuelekea hospitali kuanza mara moja na baada ya kufika Tegeta mwisho walitafuta hospitali na kuandika maelezo ili ahifadhiwe,madaktari walimpima na kuthibitisha ni kweli amefariki dunia.
“Ndio amefariki,nitaandikaje ripoti afande?”
“Andika alikufa kwenye mafuriko ya maji”
“Sawa afande”
Hakukuwa na haja ya kuuweka mwili wa Issa juu ya kitanda chenye matairi,machela ilisukumizwa moja kwa moja mpaka chumba cha kuhifadhia maiti yaani Monchwari na askari wakaondoka na mtuhumiwa waliyekuwa wanamsaka.
*** ******
Katrina alikuwa ni kama mtu aliyekuwa ana ugonjwa mbaya wa arosto,hakula chakula wala kunywa maji kwa takribani siku tatu mfululizo mwili wake ulipungua uzito kilo kumi tayari, hiyo ilitokana na mawazo juu ya Issa,hakuelewa ni wapi alipo na anafanya nini lakini moyo wake ulimuuma ajabu,hapo ndipo alipohisi kwamba huko alipo mpenzi wake anapata shida kupita kiasi.Kutokana na kukataa kula chakula ilimfanya akae hospitali kwa kipindi kirefu mno,Mama yake alimwaga machozi kila kukicha hali ya mwanaye ilimuogopesha na alijuwa fika angeendelea kukaa na njaa angepoteza maisha kama sio kuibuka na magonjwa mengine kama vidonda vya tumbo ama ‘ulcers’kwa lugha nyingine ya kitaalam!
“Mom,Issa yuko wapi?”
Hilo ndilo lilikuwa swali la Katrina kila alipozinduka kutoka usingizini na siyo hivyo tu bali Katrina alifanya fujo na kuchomoa mirija ya dripu na kila kitu, akitaka kutoka nje.Kuanzia hapo hakuna mtu mwingine aliyeweza kumtuliza isipokuwa sindano kali za usingizi.
“Hapana,usimchome tena”
Dokta Khaila aliingilia kati, kuchomwa sindano kila wakati kwa binti yake kilimchukiza na alijuwa wazi baadaye angepata madhara makubwa mno.
“Dokta sasa tufanye nini?”
Nesi akataka kujua ni hatua gani achukuwe.
“Niachie mimi”
Nesi akasitisha zoezi lake na kuendelea na kazi zake nyingine.Katrina aliendelea kupiga kelele huku akilitaja jina la Issa tu.
“Katrina mwanangu nisikilize”
“Hapana Mom,siwezi kukusikiliza.Namtaka Issa,niambie ukweli kama amekufa”
“Hapana hajafa”
“Yuko wapi sasa?”
“Sijui”
“Kwanini usijuwe Mom,niambie ukweli mimi nitajiua”
Katika maongezi ya Katrina hakuonesha aina yoyote ile ya utani na alikuwa ana kila sababu ya kusema hivyo sababu ya mapenzi mazito aliyokuwa nayo moyoni mwake.
“Katrina usifike huko”
“Issa yuko wapi?”
“Ngoja nikamuulize Baba yako,nisubiri hapo”
“Namimi nakuja”
“Katrina subiri kitandani”
Haikuwa kazi rahisi hata kidogo kumtuliza Katrina aliyekuwa anabishana na Mama yake mzazi, kwa mambo aliyokuwa anayafanya hata yeye alijishangaa mwenyewe,alihisi moyo wake unataka kumuona Issa.
Kwa hofu ya binti yake kujinyonga Dokta Khaila akatoka wodini moja kwa moja na kunyoosha mpaka kwa mume wake ambaye alimkuta ameinamisha kichwa chake chini hiyo ilionesha ni jinsi gani alikuwa ana mawazo mengi.
“Kapoor”
“Kapoor”
“Kapoor”
Dokta Khaila aliita lakini hakujibiwa,Kichwa cha Dokta Kapoor kilikuwa juu ya meza ni wazi kwamba alikuwa ana mawazo kuliko kawaida na kichwa chake kilikuwa kizito zaidi ya ndoo iliyokuwa na zege, hiyo ilisababishwa na mawazo tele!
“Kapoor”
Mpaka mkewe anamsogelea na kumuita hakuweza kumsikia mpaka alivyoguswa begani,taratibu akainua shingo na kumtizama Dokta Khaila.
“Unawaza nini?”
Dokta Khaila akaanza kuhoji.
“Nina matatizo makubwa sana”
“Yapi hayo?”
“Katrina anaendeleaje?”
Dokta Kapoor akabadili mada hapohapo, hakutaka kuweka matatizo yake wazi na kumwambia mkewe.
“Ndio maana nimekufuata,Issa yuko wapi?”
“Issa,Issa yupo.Yupo mbali kidogo ataletwa”
“Kila siku yupo mbali?Mbona sikuelewi Kapoor,Katrina hajala leo siku ya tatu.Unategemea nini?”
Lilikuwa ni swali lingine kutoka kwa Mkewe lakini kwa sauti ya ukali kidogo.
“Yupo”
“Yupo,yupo wapi?Kila siku unaniambia yupo,kila nikikuuliza unaniambia yupo.Mbona hutaki kuniweka wazi?Kama umemuuwa niambie tu”
Dokta Khaila akapandisha hasira na kuanza kumfokea mume wake akimkaripia,majibu aliyokuwa anapewa kila siku na kupigwa kalenda yalimchosha na alifanya hivyo sababu alitaka Katrina apone.
Na ukweli ni kwamba maisha ya Katrina yalikuwa mikononi mwa Issa na kwa wakati huo Dokta Kapoor hakuelewa ni wapi Issa alipo hiyo ndiyo ilimfanya ababaike kutoa jibu lililonyooka kwa mkewe,aliogopa.
“Darling punguza jazba”
“Hapana siwezi”
“Nataka nikwambie ukweli”
“Sema sasa,amekufa?”
“Hapana”
“Sasa mbona husemi alipo,yuko wapi?”
“Sijui alipo”
“Kapoor,mbona sikuelewi.Acha mambo ya kitoto”
Dokta Kapoor akashusha pumzi ya kuchoka na kutoa miwani yake machoni,akamtizama mkewe kwa kitambo kidogo.
“Kaa kwenye kiti basi”
“Sawa,lakini niambie Issa alipo”
“Ni stori ndefu kidogo”
Hakukuwa na haja tena ya kubaki na siri hiyo ndani ya mtima wake,Dokta Kapoor akafunguka na kusema mkasa wote uliotokea mpaka ajali ilivyotokea na watu wote kufariki dunia wakiwa na siri ya wapi Issa alipo.
Jambo hilo kwa Dokta Khaila lilitisha kupita kiasi, hakuelewa ni kwa namna gani atoe jibu sababu hata yeye aliishiwa pozi,hakuna hata mmoja kati yao aliyejuwa kuwa Issa yupo shimoni anapigania maisha yake.
“Lakini tutampata Darling”
Dokta Kapoor akajaribu kumpa mke wake moyo lakini hiyo haikusaidia chochote kile.
“Nina uhakika ameshakufa,uliniambia alitupwa kwenye shimo”
“Ndio”
“Oh My God”(Mungu wangu)
Dokta Khaila alinyong’onyea na alichoka akili mpaka mwili mzima.
“Doktaaaa doktaaaaaa doktaaaaa”
Sauti ya nesi aliyekuwa anamuangalia Katrina ndiyo iliyosikika ikiita kutokea kwenye kordo ya hospitali na hiyo ndiyo iliwafanya Dokta Kapoor na mkewe wasimame wima kwa pamoja na kuanza kugombea mlango kutoka nje hiyo ikawapelekea mpaka wapigane vikumbo sababu kulikuwa kuna kila dalili ya habari mbaya.
“Subi kuna nini?”
Dokta Khaila akamshika mkono nesi na kumtandika swali.
“Katrina..Katri..na”
“Kafanya nini?”
“Ame…..”
Kuendelea kumuhoji Nesi Subi maswali isingesaidia chochote,Dokta Khaila akamuacha hapohapo na kuanza kukimbia ambapo mumewe alikuwa mbele yake,moyoni aliomba sana asikute jambo ambalo analiwaza,alivyoufikia mlango akazama ndani moja kwa moja ambapo alikumbana na lundo la madaktari zaidi ya tisa,picha aliyoiona ilimuogopesha kwa kiasi cha kutosha.Katrina alikuwa ameshika kisu mikononi mwake na makali kayaelekezea juu ya tumbo lake.Ni wazi kwamba mtoto huyu aliwaweka watu roho juu na alidhamiria kufa,mikono yake ilishikwa na madaktari watatu wakijaribu kushindana naye nguvu na kutaka kumnyang’anya kisu alichokuwa nacho mikononi kwake,kumuachia kulimaanisha utumbo wa Katrina kuwa nje na huo ndio ungekuwa mwisho wake duniani.
“Namta…kaa Issa…aa”
Hivyo ndivyo alikuwa akisema Katrina huku akiwa ameshika kisu mikononi mwake anakivuta kukindamiza juu ya tumbo lake,hakuwa ana sababu ya kuishi duniani bila ya Issa, mwanaume aliyemtoa bikira yake na isitoshe alimpenda kupita maelezo yaliyojitosheleza.
Habari za watu kujiua katika mapenzi alishawahi kuzisikia na kuthubutu kusema kwamba ni wapumbavu leo hii aliamini ni kweli mapenzi yanauwa na yanauma vibaya,ni wazi kwamba Katrina alikuwa mwenye moyo mwepesi kupita kiasi.Hakuna daktari hata mmoja aliyejuwa Issa ni nani isipokuwa Dokta Khaila na mumewe!
***********
“Tabiaaa ya mpemba yuleeee ilikuwa kawaaidaaaa,mwenye nyumbaaaa,kagunduaaa kila kituuuu..Pwapwaa pwaaa pwaaa pwaaaaa.Hizi kazi zingine basi tu sababu sina elimu,kazi gani hizi za kulinda maitiii,anyway bullshit never mind hawa ni ndugu zangu.Nyie maiti”Sauti kutokea chumba kinachohifadhiwa maiti ilisikika ikiimba na mtu anazungumza mwenyewe!
Alikuwa ni mzee mwenye umri kati ya miaka 60-70,maisha yake yote alikuwa akikaa na maiti akizilinda monchwari kama akihamishwa hospitali hii basi anapelekwa mkoa mwingine.Hakuweza kufanya hivyo bila kupiga kileo ama kuvuta bangi,Mzee Jungu alikuwa akinywa kiasi kingi cha pombe kabla ya kufika kazini kwake na wakati mwingi alitumia pombe kali za kienyeji kama gongo, chang’aa ama mnazi aliamini kwa kufanya hivyo hatohofia chochote wala hatoogopa mauzauza ya aina yoyote ile, mbali na hapo aliipenda kazi yake sababu ndiyo iliyomfanya aishi na kula!
“Laaakiiiiiini leooo baridiii kidogooo,sasa Washkaji zanguuuu eeeh mimi nawalinda nipo hapa,kamanda Jungu”
Mzee Jungu aliendelea kuzungumza na maiti ilihali alijuwa hatojibiwa.

***************

Kwa mbali alianza kuhisi baridi kali mno na mwili wake ulikuwa umekufa ganzi,akajaribu kuvuta kumbukumbu lakini ziligoma kukaa sawa kabisa.Bado hakuelewa yupo eneo gani lakini baada ya sekunde kama ishirini hivi akili zake zikaanza kujikusanya taratibu, akaona jinsi alivyotupwa ndani ya shimo na baadaye mvua kubwa kunyesha,akasikia milio ya risasi kuanzia hapo hakuelewa kilichoendelea.Alivyojaribu kufumbua macho alikumbana na giza nene,hakuweza kuona mbele lakini alichohisi yeye ni ubaridi unampuliza.Akajaribu kujigeuza lakini akashindwa,akasogeza mguu wake mpaka mwisho,akahisi amegusa kitu kama chenye ubaridi,alivyorudisha kichwa chake nyuma akajigonga na mwangaza ukatokeza,akajisukuma zaidi kwa nyuma,friji likafunguka akadondoka chini puuu kama gunia na kuanza kujivuta.
“Mtumeeeeeeeeeee,tobaa yarabiiii.Yesuu na mtumeee,nafwaaaa”
Mzee Jungu alishtuka kuona maiti imetoka ndani ya friji na imeanza kusogea, nguvu zilimuishia kwa uwoga na hofu alijikuta anajikojolea na kutoa haja kubwa kwa wakati mmoja.



Tangu aanze kufanya kazi yake ya kulinda maiti hakuwahi kukutana na tukio hilo la ajabu tena la kutisha,Mzee Jungu alitetemeka kwa kiasi cha kutosha nguo zake zilikuwa tayari zimelowana kwa mkojo na kinyesi,alivyotaka kusimama hakuweza sababu hakuwa na nguvu hata moja.Akajikakamua na kujizoa,alivyokaa sawa hakutaka kugeuka nyuma alianza kukimbia lakini alivyofika mlangoni aliteleza na kudondoka chali sakafuni.
Bado Issa hakuelewa ni wapi alipo lakini alivyotuliza mawazo aligundua,hakuwa ana nguvu hata ya kusimama na kutembea bado alikuwa dhaifu sababu ya njaa kali na kiu alivyokuwa navyo,alivyokumbuka kifo alichokoswa nacho hapohapo nguvu zilimjia ghafla, alijuwa fika kwamba bado Mzee Kapoor anamsaka na anahitajika auliwe hivyo kubaki mahali hapo ilimaanisha kukisubiri kifo chake.Akaanza kutembea kwa kupepesuka lakini alivyojiangalia vizuri akagundua kwamba hakuwa na nguo yoyote ile,akatembea mpaka kwa mlinzi aliyekuwa chini hana nguvu macho yanamtoka,akajuwa tayari siku hiyo analiwa nyama mzima mzima hiyo ilimfanya mlinzi agande kama barafu.Alichofanya Issa ni kumvua nguo zake na hakutaka kujali zina uchafu kiasi gani alichotaka yeye ni kujistili,akaziweka mwilini na kufungua mlango na kuanza kutembea huku akipepesuka.Alivyohakikisha ametoka nje ya hospitali kwa tahadhari tena bila ya kushtukiwa alisimama nyuma ya ukuta na kuanza kutafakari.
Akili yake ilishindwa kufanya kazi kabisa lakini alivyojisachi mfukoni alikumbana na noti noti akazitoa haraka,zilikuwa ni pesa.Kutokana na njaa aliyokuwa nayo kitu kilichomjia kichwani ni kunyoosha moja kwa moja mpaka kwa Mama nt’ilie, hapo aliagiza wali sahani tatu kwa mpigo,kila mtu ndani ya mgahawa huo alimshangaa,Issa hakujali alichotaka yeye ni kujitetea kwa kuweka tumbo lake sawa,siku hiyo alikula harakaharaka na kupiga matonge makubwa ya ubwabwa, sahani mbili zikaisha kwa dakika mbili na alivyomaliza sahani ya tatu alinunua maji ya kunywa.Macho ya wateja mpaka Mama nt’ilie yote yalikuwa kwake.Akalipa pesa na kuondoka zake,hakutaka kwenda sehemu nyingine zaidi ya kukimbilia Manzese aliamini huko ndipo ingekuwa ponea yake,aliwakumbuka sana marafiki zake.Kitu ambacho kilimuogopesha zaidi ni sura ya Mzee Kapoor hiyo ilimfanya mpaka ajishtukie kila akikumbana na watu wanamwangalia sababu alijuwa kivyovyote vile ni lazima mzee Kapoor kawatuma watu wake wamemtafute.
Kwa uwoga hivyo hivyo alifanikiwa kupanda daladala na alivyoteremka Ubungo akaanza kuchapa mguu mpaka alipofika Shekilango hapo akazidi kusonga mbele zaidi na kwa mbali aliona daraja la Manzese hiyo ilimtia moyo zaidi na kumfanya azidi kutembea kwa haraka sana.
Kama kawaida ya Manzese na hekaheka zake ndivyo ilivyokuwa siku hiyo,mitumba iliyokuwa inauzwa ilimkumbusha vitu vingi katika maisha yake hususani Marietha.Hakutaka kumkumbuka katika maisha yake sababu aliamini kwamba ndiye mkandarasi wa matatizo yote yaliyotokea katika maisha yake,akapangua pangua watu akafika mpaka kwenye goli analouza kishipa.
“Kishiiipa,Kishiiiipa”
Issa aliita kwa sauti ya chini,aliogopa kuonwa na watu wengi!
“Issaaaaaaaa”
Kishipa aliropoka kwa sauti kubwa na kuacha anachokifanya mtu aliyekuwa mbele yake alimuogopesha kupita kiasi na alimshtua kiujumla.Mbali na hapo Issa alikuwa ana makovu usoni hilo likaibua swali lingine kutoka kwa kishipa.
“Kishipa naomba funguo za geto lako”
“Issa ulikuwa wapi?”
“Ni hadithi ndefu rafiki yangu”
“Issa ni wewee kweli?Usoni umefanya nini?”
“Ni stori ndefu nitakwambia”
“Ulipata ajali au?”
Ni wazi kwamba Issa hakuwa tayari kuongea chochote kwa wakati huo.Alitaka kupumzika kwanza na alisisitiza apewe funguo,alivyopewa alitembea kwa haraka,kwa kuwa geto la Kishipa alilijuwa hilo halikumpa shida yoyote ile,alivyofika tu aliingiza funguo kwenye kitasa na kukinyonga,akazama ndani ya chumba cha Kishipa,kilikuwa ni chumba kidogo chenye dirisha moja peke yake.Bado Issa hakuamini kama amenusurika kifo kwa mara nyingine,aliamini kwamba bado Mungu anapigania uhai wake.Alichofanya ni kujifungia kwa ndani sababu alihisi bado anatafutwa na watu wa mzee Kapoor.
Baadaye kidogo mlango ukagongwa,hata hivyo hakufungua aliliendea dirisha na kuchungulia ndipo alipouendea mlango baada ya kumuona Kishipa.
“Vipi?”
Kishipa akataka kujua kiundani zaidi.Issa hakuwa ana sababu yoyote ile ya kuweka mambo ndani ya kifua chake,akasema kila kitu kilichotokea katika maisha yake mpaka akajikuta yupo Monchwari na mwisho akahitimisha kwamba uwepo wake hapo uwe siri kubwa.
Historia ya Issa ilisikitisha na ilikuwa ya kuuzunisha, Kishipa alimuonea sana huruma swaiba wake,akamuhaidi kwamba atafanya hivyo siku zote na hakuna mtu yoyote yule atakaye juwa kwamba Issa yupo mahali hapo.
“Umekula?”
Kishipa akauliza.
“Ndio”
“Basi wewe poa hapa,mimi nitakuja baadaye.Usifungue mlango kwa mtu yoyote yule isipokuwa mimi”
“Poa Kishipa,Ahsante”
Issa na Kishipa walikuwa ni marafiki wa kufa na kuzikana.Ni wazi kwamba walitoka mbali na hata kama Kishipa angewekewa bastola kichwani habadani asingeweza kusema ni wapi Issa alipo.
Maisha ya Issa yalikuwa ya kukaa ndani kama mwali,aliletewa chakula na maji akiwa humohumo chumbani ama magetoni na alitoka nje usiku kwa usiku tena kutoa haja na kuoga kisha kurudi mafichoni hiyo yote ilikuwa ni kuiokoa nafsi yake,kuonekana nje kulimaanisha kifo chake na kwa hilo hakutaka litokee ingawa hakuelewa mwisho wa maisha yake utakuwa nini.
*****************

Sio Mzee Kapoor wala mkewe Dokta Khaila wote walikuwa wenye mawazo kupita kiasi,walishindwa kuelewa ni kwa namna gani wamsaidie binti yao ili aweze kutulia.Sio kwamba hawakujuwa kuwa Issa ndiyo mwisho wa yote la hasha,bali hawakujuwa ni wapi alipo na walikuwa wana uhakika asilimia mia moja kwamba mwili wake upo mahali fulani tena ndani ya shimo refu na tayari ni maiti.Kila mtu alianza kumtupia mwenzake lawama na walitamani siku zirudi nyuma wabadilishe mambo lakini haikuwa hivyo kwani muda hauwezi kurudi nyuma hata kidogo.Katrina aliendelea kuwatesa na aligoma kula mbali na hapo alitaka kujiua na zisingekuwa juhudi za madaktari kumpokonya kisu siku hiyo wenda wangekuwa wanazungumzia habari nyingine za msiba!
“Inawezekana Issa hajafa”
Dokta Khaila akaropoka akimwambia mumewe, kuna kitu ilionekana alitaka kujaribu kukifanya.
“Hajafa?Una maana gani?”
“Si ulimwacha kwenye shimo?”
“Ndio”
“Kwanini tusijaribu kutuma watu kusaka mashimo yote hapa Dar es salaam”
Jiji la Dar es salaam lilikuwa kubwa mno na haikuwezekana kumsaka mtu kwa staili aliyoshauri Dokta Khaila,bado wazo lake halikusaidia ingawa alitaka iwe hivyo kwani kumpata Issa ilikuwa ndiyo njia pekee ya kumtuliza Katrina.
“Hapana tutapoteza pesa zetu bure”
“Kwahiyo pesa kwako muhimu kuliko mtoto wetu?”
“Sina maana hiyo”
“Una maana gani labda?”
“Kuanza kutafuta mashimo jiji zima hiyo kazi haitoisha leo”
“Hata kama haitoisha leo lakini tulifanikishe swala hilo”
“Sasa kama tayari amekufa?”
“Bora tujue hivyo”
Dokta Khaila na mumewe walikuwa kwenye mjadala mdogo lakini mzito ambao ulifanyika kwa siri kubwa mno ndani ya ofisi yao mlango ukiwa umefungwa,kama maongezi yao yangesikiwa basi gereza lingewahusu katika kubishana kwao walifikia muafaka kwamba watume watu chini kwa chini waende Monchwari zote kutafuta mwili wa Issa japokuwa wazo hilo halikuwa na nguvu sana!
Kazi ilianza mara moja mzee Kapoor akachota kiasi kingi cha pesa kwenye akaunti yake na kuwaita vijana wa kazi,kila mtu akapewa kibarua hiko.
Kazi hiyo ilifanywa na vijana sita tu kwa maana hiyo walijigawa wawili wawili kila mmoja akiwa na picha.Wengine walienda hospitali za wilaya ya Ilala na baadhi wakazuka wilaya ya Kinondoni na wawili waliobaki wao waliingia hospitali za wilaya ya Temeke, haikuwa kazi ya kitoto.Kazi ikaanza mara moja,vijana wakaingia mzigoni baada ya kupewa nusu ya malipo ya pesa zao na salio lililobaki ilitakiwa wamaliziwe baada ya kazi.Siku saba baadaye ripoti waliyoleta haikuwa nzuri,hakuna hata mmoja kati yao aliyekuwa na taarifa ya kuridhisha!Hiyo iliwavunja moyo sana Dokta Khaila na Mumewe,walichukulia moja kwa moja kwamba Issa alikufa ndani ya shimo kwa kufukiwa na kifusi.
Seble ilitawaliwa na ukimnya, Sio Dokta Khaila wala Mkewe pamoja na vijana wa kazi.Kwa kuwa mzee Kapoor aliwahaidi atawalipa pesa zao hakuwa na jinsi kila mmoja alim-malizia pesa yake kisha kuondoka zao,akabaki yeye na mkewe.
“Sasa tutafanya nini?”
Dokta Khaila akaibuka na swali ambalo lilikosa jibu.
“Wacha nifikirie kitu gani nifanye,piga simu hospitali ujue hali ya Katrina”
Dokta Kapoor alitaka kupumzisha kwanza akili yake ili ajuwe ni kitu gani akifanye,alitembea mpaka chumbani kwake na kujitupa kitandani, bado alikuwa akitafakari mambo mbalimbali na maisha yake kiujumla na kilichomnyima raha ya maisha ni biashara yake chafu ya kuuza figo za binadamu wenzake.Simu alizokuwa anapigiwa na maaskari mbalimbali zilimuogopesha na ilionekasna alikuwa akichunguzwa mno.hilo ndilo lilimtisha zaidi na zaidi.Katika kuwaza kwake na kuwa mbali kimawazo simu yake ya mkononi ilimshtua na ilikuwa namba ngeni,akaichukuwa na kuiweka sikioni baada ya kuipokea!
“Halloo Mr.Kapoor”
“Ndio nani veve?”
Mzee Kapoor alitaka kujuwa mtu anayezungumza naye kabla ya mambo mengine kuendelea mbele zaidi.
“Mimi yule kijana wako Gadagada”
“Gadagada,wa wapi?Zungumza kwa sauti hapana potezea muda mimi”
“Ni mmoja wa vijana uliotutuma kumtamfa Issa”
“Sema,ndio ulikuwa taka nini?”
“Kuna kitu nataka kukwambia”
“Kitu gani?”
“Ninajuwa wapi pa kumpata Issa”
“Sema nini wewe?”
“Nina juwa Issa alipo”
“Iko wapi?”
“Nitumie kwanza pesa”
“Hapana ninajuwa ninyi vijana wa mjini ni wahuni sana.Nataka ona Issa kwanza kisha nikupe wewe Pesa”
“Sawa,kesho asubuhi”
“Hapana fanya sasa hivi.Wewe iko wapi?”
“Nipo hapa Vingunguti”
“Chukuwa pikipiki njoo kwangu Oysterbay”
“Sawa mzee”
Simu ilivyokatwa ilimuacha Mzee Kapoor anakaa kitako,habari za Issa kuonekana zilirudisha matumaini yake upya akatoka chumbani na kumpasha mke wake kile alichoambiwa simuni,Kwa Dokta Khaila hizo kwake zilikuwa habari njema sana.Dakika ishirini baadaye Kijana akagonga geti na kukaribishwa ndani bila kupoteza muda akaanza kuhadithia mkasa mzima kinagaubaga.
“Ulisema uliambiwa na mlinzi anayelinda monchwari?”
Dokta Khaila alihoji huku akimtizama kijana machoni.
“Ndio,hospitali ya Tegeta”
“Una uhakika?”
“Hilo nina uhakika nalo na daktari aliyempima amethibitisha hilo baada ya kumpa picha”
“Una uhakika?”
“Ndio”
“Subiri”
Haikuwa kazi ngumu kwa madaktari kujuana,Umaarufu wa Dokta Khaila ulifanya ajuane na madaktari wengi kwenye mahospitali makubwa.Alitembea mpaka chumbani na kutafuta ‘diary’yake akaifungua mpaka alipolifikia jina la Dokta Sabihi.Akaiweka juu ya simu yake na kuruka hewani hapohapo.Dokta Mariam Sabihi alikuwa daktari bingwa katika hospitali ya serikali huko Tegeta na kwa kumtafuta yeye aliamini kwamba kuna vitu atavijuwa,ni kweli kuna kitu aliambiwa.
“Tukio lilitokea kama three weeks back!Dokta Othman aliletewa mgonjwa na maaskari akampima akagundua kwamba amekufa,kumbe haikuwa hivyo alikuwa amelewa pombe na alimpima harakaharaka kijana ilivyofika asubuhi nadhani alipata fahamu.Hio habari hukuisikia kwani?Imezungumziwa sana kwenye Redio na T.v”
“Huyo kijana anafananaje?”
“Kwa kweli sijui vizuri sababu hata mimi sikumuona kwa macho yangu”
“Dokta Othman sasa hivi yuko wapi?”
“Kafukuzwa kazi”
“Nitumie namba zake”
“Sawa,ninakutumia sasa hivi”
Simu ilivyokatwa hapohapo namba ikatumwa kwa njia ya meseji.Dokta Khaila bila kupoteza wakati akaruka hewani,ni kweli kwamba kitu alichoambiwa hakikuwa fununu bali ni kweli kwamba kuna mtu alizinduka kutoka chumba cha kuhifadhia maiti.Akazidi kumuhoji maswali dokta Othman na baadaye akagundua kuwa ni kweli alikuwa ni Issa.
“Okay ahsante”
Simu ikakatwa na kilichofuata hapo ni kuanza kupanga mikakati ya kumsaka Issa kwa wudi na Uvumba wakiamini kwamba ndio suluisho la Katrina kupona.



Siku hiyo usiku simu zilikuwa bize kwa kiasi cha kutosha,Dokta Khaila alikuwa ana kazi ya kuwapigia waandishi wa habari mbalimbali ili watangaze kumsaka Issa hivyohivyo pia alifanya Dokta Kapoor bila kuchoka ni wazi kwamba alikuwa tayari kufanya hivyo ili binti yake apone lakini vinginevyo Issa angekuwa kitoweo chake,hasira zote ziliyeyuka jambo lililotakiwa kufanyika ni kuokoa maisha ya binti yake,ndiyo maana alihaha sababu Katrina alikuwa kama mboni ya jicho lake siku zote.Mpaka kunapambazuka walifanikiwa kuwapigia waandishi tofauti tofauti kama Emma Mlawa wa Clouds t.v. Mwandishi Victor John,Octavian Kessy na wengine wengi wakubwa.Pesa zikatumwa pamoja na picha ya Issa Nurdin Mpelembe,siku hiyo kila chombo cha habari kilirushwa picha ya Issa akiwa anatafutwa,habari zikawa zimesambaa kwa kasi ya umeme jiji zima la Dar es salaam na mikoa jirani kama Pwani,Morogoro,Tanga,Dodoma na Arusha sio hapo tu habari zake zilienea kwenye vyombo vya habari vikisema kwamba ‘MTOTO WA TAJIRI APOTEA’ hivyo ndivyo hata kwenye magazeti waliandika huku picha yake ikiwa juu,baada ya kuhakikisha zoezi hilo limekamilika wakitegemea watapata majibu mazuri lakini wapi,dalili ya Issa kuonekana hazikuwepo hata kidogo,hiyo iliwafanya wazidi kuchanganyikiwa sababu mwili wa Katrina uliporomoka kupita kiasi,hakutaka kula kitu chochote mpaka wakati mwingine madaktari walitumia nguvu kumlisha lakini matokeo yake alibana meno,ukweli ni kwamba alidhamiria kufa.Tayari alishaelewa kwamba Issa ameshakufa na kuwepo duniani bila Issa kwake swala hilo alilichukulia ni kama usaliti wa hali ya juu sana sababu kifo cha Issa yeye ndiye aliyekisababisha.Ungepewa picha ya Katrina na kuambiwa ndiye msichana aliyelala kitandani habadani ungebisha,mashavu yake yaliingia ndani,midomo ilikuwa imemkauka kama kaukau!
Kifupi hakutofautishwa na mgonjwa wa Kifua kikuu.Dokta Khaila aliumia moyo na Mzee Kapoor machozi yalimlenga ukweli ulikuwa wazi kwamba Katrina asingefikisha siku nne mbele angekufa kwa njaa tena ya mateso.
Katrina alihisi maumivu ya hali ya juu lakini hakujali,alitaka kufa na alitaka kutumia njia hiyo sababu hakuwa na mbinu nyingine zaidi, hakutaka kujali ni kiasi gani anawaumiza wazazi wake,alichotaka yeye ni kumfuata Issa wake huko ahera.
“Ma…ma ni..nak..ufa.Ninamfu..ata Issa,na..ku..penda sa..na”
Hayo ndiyo maneno aliyokuwa anasema Katrina huku chozi moja likimtoka,kifo alikiona mbele yake ndiyo maana akasema vitu kama hivyo vizito,utumbo wake haukuwa na kitu hata kidogo hiyo ilimfanya awe dhaifu kuliko kawaida.
“Katrina mwanangu,jitahidi ule.Issa yupo hai tunafanya jitihada za kumtafuta”
“Ha…pana sio u..kweli.Ache..ni nif..e nipo tay..ri buli..ani Mama”
Mama alimwaga machozi kama mtoto mdogo na alimlilia binti yake,kama angefariki siku yoyote ile sidhani kama angejisamehe sababu yeye ndiye alikuwa chanzo kwa njia moja ama nyingine!Hakujali kwamba analia mbele ya wafanyakazi wake,mtu kama yeye mwenye wadhifa alitakiwa kujifungia chumbani ama kuingia bafuni ndio alie lakini ilikuwa tofauti kwani alimwaga machozi mbele ya kadamnasi,kila daktari aliyeingia alimuonea huruma sana!
Wakati Katrina yupo kitandani anasubiri kifo chake huko mjini Mzee Kapoor alikuwa anahangaika na waandishi wa habari ili wazidi kumsaka Issa,alimwaga takribani jumla ya shilingi milino Saba za kitanzania mpaka siku hiyo lakini hakukuwa na dalili yoyote ile,ikabidi watumie njia nyingine mbadala.
Kibarua kikabadilika Issa akawa anatafutwa kwa dau kubwa la shilingi milioni tano.Atakayempata pesa ilikuwa halali yake,hapo ndipo watu wakaanza kulitilia tangazo hilo maanani na kutokana na hali ilivyokuwa ngumu kimaisha kila raia alikuwa makini na mwenzake.
Siku mbili zikapita lakini wapi,Dokta Khaila nayeye akaweka million kumi ikawa jumla shilingi milioni kumi na tano.Issa akageuka na kuwa almasi na kila mtu alitamani amkamate ili ajikwamue na umaskini.Jiji Dar es salaam lilipekuliwa nje-ndani,ndani ya daladala abiria walitizamana usoni kwa makini na kila mtu akawa anamchunguza mwenzake mara mbilimbili.
************
Sio kwamba Issa hakujuwa kuwa anasakwa kwa wudi na uvumba la hasha,habari hizo alizisikia na aliendelea kujificha ndani ya chumba cha Kishipa akiwa mwenye hofu,alielewa kuonekana kwake ndio ungekuwa mwisho wake na alijuwa tayari siku zake zinahesabika kutokana na pesa nyingi zilizotangazwa kama dau,hiyo ndiyo ikamtia uwoga zaidi.Licha ya hayo yote kuzungumziwa ama kutangazwa dau lakini kishipa aliendelea kumficha rafiki yake,hakutaka kumuuza kama alivyofanya Yuda Escarliot kwa Yesu,kwake pesa haikuwa kitu kabisa na hiyo ilikuwa wazi kutoka moyoni mwake na hata kama angepewa mabilioni ya pesa aseme ni wapi Issa alipo asingefungua mdomo wake habadani na ndiyo maana kila aliposikia tangazo alimfuata Issa na kumwambia ukweli.
“Unatafutwa ndugu yangu,unasakwa sana.Kwenye magazeti kote kuna picha zako,leo nimesikia tena kwenye redio.Ulimfanya nini yule mzee?”
Kishipa alikuwa anampasha Issa siku hiyo jioni alivyotoka kwenye shughuli zake za kuuza mitumba alikuwa ana kila sababu na kumuweka wazi na kumkinga dhidi ya watu wabaya wanaomsaka.
“Sio kitu bali ni Katrina tu.Nilitembea na binti yake”
“Haiwezekani,kuna kitu ulifanya”
“Niamini Kishipa,ninakuomba usimwambie mtu yoyote yule kama mimi nipo hapa”
“Hilo siwezi kusema lakini kwa ushauri wangu hapa sio salama”
“Naelewa”
“Inabidi nikutafutie japo nauli kidogo ili ukimbie mbali kabisa.Maana sasa hivi topic niwewe,kila mtu anataka hizo milioni kumi na tano”
Haikuwa utani!Issa ndiye alikuwa ‘topic’ ya jiji zima,kwa jinsi mambo yalivyoenda alijuwa kuwa wanamsaka ili wamuuwe na sio kumtibu mpenzi wake Katrina ambaye alikuwa kitandani hoi maututi anataka kufa kwa ajili yake,laiti angelijua hilo angejitokeza mara moja lakini badala yake alijificha na hakuwa tayari kujitokeza sababu aliogopa kifo kibaya,ilikuwa ni bora kuraruliwa na simba ama kutafunwa na mamba kuliko kukumbana na Mzee huyu hatari, Kapoor!
Mbali na kutangazwa katika vyombo vya habari na mitandaoni kote hawakufanikiwa kumpata hata siku moja,hawakuelewa hata siku moja kama Issa yupo Manzese amejificha, siri hiyo alikuwa nayo Kishipa peke yake na alikuwa tayari kufa nayo.Hakuwa tayari kumwambia mtu yoyote yule kitu kama hicho sababu alilifananisha swala hilo ni unafki na usaliti na asingeweza kufanya hivyo kwa rafiki yake,aliapia.
“Issa unatafutwa lakini nina kuhakikishia kwamba hakuna mtu yoyote atakayejua upo mahali hapa labda niwe nimekufa wewe ni rafiki yangu,bora nife mimi”
Kishipa alimwambia Issa siku hiyo usiku.
“Lakini kama nilivyokwambia hapa uhame sio sehemu salama”
“Sasa nitaenda wapi?”
“Kuna rafiki yangu mmoja anaishi Kivule kule nataka uende,ukakae mpaka hali itulie”
“Ahsante sana Kishipa”
“Usijali sana shika hii elfu kumi.Tusubiri mpaka usiku uingie”
Kishipa alikuwa mwenye nia ya kumsaidia rafiki yake tena kwa moyo mmoja kabisa.
Usiku wa siku hiyo ilibidi amtoe eneo hilo la Manzese na kumpeleka sehemu nyingine kabisa.Safari ya kutolewa Kwa Issa usiku haikutofautishwa na watu wanaosafirisha magendo,mlango ulifunguliwa saa saba za usiku kabla ya kuanza kutoka nje Kishipa alichungulia nje kama kuna usalama wa kutoka,Issa alikuwa nyuma amejifunika vitambaa usoni ili kuziba sura yake,alielewa nini maana ya kugundulika.
Kila kitu kilivyokuwa sawa na Kishipa alivyoona kuna usalama wakaanza kutoka nje kwa tahadhari kubwa mno.Wakatembea mpaka walivyofika stendi ya basi Manzese darajani,hapo walikuwa wanasubiri usafiri ili waende mbali huko Kivule kwa maana hiyo ilikuwa ni lazima wapakie daladala la Ubungo kisha baadaye wachukuwe gari zinazoenda Gongo la Mboto hapo wangeteremka Banana,hawakuwa wenye uhakika kama wangefika salama kutokana na picha zilivyokuwa nyingi za Issa kubandikwa katika kila nguzo.Issa alivyoangalia picha hizo alihisi tumbo linamuuma, hakuelewa la kuharisha au la uwoga,ilikuwa ni bora ardhi ipasuke atumbukie ndani lakini sio kuingia mikononi mwa mzee gaidi, Kapoor.
Daladala zilikuwa zikipita moja moja tena kila baada ya dakika ishirini ni kwasababu ya usiku kuingia.
“Ubungoooo hiyooo stendi ya mkoa.Vipi mnaenda?Dereva kula vichwa”
Mpiga debe alisema baada ya basi la abiria kusimama, bila kuhoji chochote Issa na Kishipa wakaingia ndani ya basi.
“Ubungo hiyo stendi ya mkoa,gari la mwisho”
Kondakta akazidi kufanya kazi yake huku akiwa anatembea tembea nje,kwa Issa na Kishipa waliokuwa wana haraka walitamani basi liondoke dakika hiyohiyo.Abiria wakaanza kuingia mmoja baada ya mwingine.
“Sio hivyo,mimi ndio nakwambia yule fala sana.Mimi ningemzingua ujue.Nina mdai pesa zangu alafu ananiletea zogo,wewe subiri mwambie nina RB yake.Mwambie hivyo na atalala Urafiki pale ashike adabu,pumbavu zake”
Hayo yalikuwa maneno ya abiria mmoja akiwa anaongea na simu tena kwa jazba,akapita pembeni ya Issa lakini alivyokaa kwenye kiti kuna kitu alikihisi,mtu aliyekuwa amejifunga matambala usoni.
“Mmmh”
Abiria huyo akaguna aliomba Mungu jambo analodhani liwe kweli ili ajikwamue katika hali ya dhiki aliyokuwa nayo.Akatembea mpaka dirishani na kuangalia picha vizuri iliyobandikwa nje ya nguzo ya umeme,akasogea na kuketi pembeni ya Issa.Akamchungulia vizuri.
“Eti samahani,hili gari la Mbagala au?”
Abiria huyo akauliza niya ilikuwa ni kuanza mazungumzo.
“Sio muulize Konda”
Kishipa ndiye aliyedakia japokuwa hakuulizwa yeye.
“Anyway.Mambo vipi?”
“Kaka embu fanya mambo yako bwana”
Kishipa akaanza kuwa mkali.
“Mnaelekea wapi?”Abiria huyo akauliza tena huku akisogea karibu zaidi.
Kwa kasi ya mwewe akavuta kitambaa kilichokuwa usoni kwa Issa.Na tayari sura yake ilikuwa wazi Kishipa alipojaribu kuleta fujo alitulizwa na kifuti cha tumbo,kumuachia Issa aondoke ilikuwa ni sawa na kuziacha milioni kumi na tano.Issa alivyotaka kukimbia akatulizwa kwenye kiti.
“Tulia kijana,watu hatuna pesa sasa hivi”
Ugomvi huo wa sekunde tatu ulifanya abiria waliokaa kugundua kwamba kijana aliyekuwa anatafutwa yupo ndani ya basi.
“Kuna nini hapo?”
Mzee mmoja akasimama wima kutoka siti ya nyuma.
“Huyu mtuhumiwa wangu,aliniibia pesa zangu”
“Kwanini usimpeleke polisi?”
“Hapana,kasema atanilipa ndio ninampeleka nyumbani”
Akadanganya!
“Mimi ni afsa wa polisi,inabidi sheria ifate mkondo wake.Mlete hapa”
“Hapana afande”
“Kwahiyo unakiuka amri ya jeshi la polisi?”
Sio kwamba Mzee huyo alikuwa polisi,aliigundua Sura ya Issa nayeye alizitaka milioni Kumi na tano, ndiyo maana akaanza kupiga mkwara hapo ndipo kila mtu macho yakawa kwa Issa,milioni kumi na tano hazikuwa ndogo.
“Nimesema hivi twende kituoni kijana,simama upesi jambazi wewe”
Mzee aliyejifanya askari akaanza kuongea kwa sauti.
“Embu simama kabla sijakupiga risasi za kichwa hapahapa,tapeli wewe.Sasa kijana mtu wako uje kumfuata pale Manzese Central”
Issa akakamatwa mkono,moyoni alikuwa mwenye hofu kupita kiasi,Kishipa alikuwa pembeni kifuti alichopigwa ilielekea kilimwingia mpaka ndani ya mfupa na kutokana na afya yake kuwa mgogoro hakuweza kuinuka tena.
“Ebwana twende”
“Mimi sio jambazi”
“Tulia hapo”
Issa akashushwa nje ya basi na Mzee huyo akaanza kutembea naye mpaka kandokando kabisa kwenye giza.
“Ukikimbia nakupiga risasi,tulia kama unaogeshwa”
Ukweli ni kwamba Mzee huyo hakuwa ana bastola yoyote ile mkwara wake ulimsaidia,moyoni alifurahi na hapohapo akatoa simu ya mkononi kisha kuanza kuangalia juu ya nguzo ambapo hapo kulikuwa na namba za simu!Hakupoteza wakati,akaruka hewani simu ikaanza kuita, moyo wake ulikuwa ukidunda kwa nguvu.
“Hallooo,unaongea na Mrema.Yule kijana ninae hapa tayari”
Mzee Mrema aliongea bila breki.
“Zungumza na nani?Kijana gani?”
Upande wa pili ulisikika kwa rafudhi ya kihindi hiyo ilimfanya Mzee Mrema asitishe mazungumzo akahisi wenda amekosea namba.
“Mimi naiitwa Mrema,Issa ninaye hapa.Nipo hapa Manzese,zile pesa nitapata?”
“Wewe iko wapi?Embu ongea na hii kijana”
Mzee Kapoor alikuwa ndani ya gari nyuma ya usukani anaendesha, akampatia mtu wa pembeni yake azungumze.
“Kaka,nambie.Upo wapi?”
“Hapa Manzese darajani,huo mzigo upo?”
“Mzigo upo.Unaye uyo Issa hapo?”
“Ndio nipo naye hapa.Sasa nije wapi?”
“Tusubiri hapohapo”
“Sawa”
Simu ikakatwa hapohapo,Mzee Kapoor alivyoelezwa ni wapi Issa alipo akazungusha usukani na kupanda tuta la katikati,akatokeza barabara ya upande wa pili ili kuitafuta barabara ya Samuni Jomma.
Kuwepo kwa Issa hai aliamini jela ingemuhusu na angeshtakiwa kwa kosa la utekaji nyara na hiyo ingekuwa kashfa kubwa kwa mtu kama yeye na alijifanya kumtafuta Issa kwa ajili ya Katrina lakini haikuwa hivyo kwani ilikuwa kinyume chake,ilikuwa ni lazima amzibe Issa mdomo hakujali tena uhai wa Katrina,taratibu akashusha mkono wake kwenye kiuno na kugusa kitu kigumu,ilikuwa ni bastola na alikuwa anahakikisha kama anayo.Ilikuwa ni lazima amuuwe Issa kwa njia moja ama nyingine sababu bado alikuwa ana kisasi naye hiyo ilimfanya akanyage mafuta mengi ili awahi kufika.




Siri hiyo ilikuwa ni lazima abaki nayo ndani ya kifua chake,amuuwe Issa ili amfunge mdomo kwa kufanya hivyo alielewa kwamba hakuna hata mtu mmoja angeijua siri hiyo,akazidi kusonga mbele mpaka alipofika Sinza Mapambano,akanyoosha mguu na kuendelea na safari, sio siri alitamani kufika mapema ili akutane na Issa ana kwa ana,gari halikudanganya tayari alifika mataa ya Shekilango akakunja kushoto na kunyoosha na barabara.Dakika tano baadaye alifika na kupaki gari barabarani kabisa,hakukuwa na maongezi wala hakutaka kupoteza muda akachukuwa simu yake na kumtafuta mtu aliyempigia simu,akatoa maelekezo mahali alipo na baada ya sekunde saba aliwaona wanaume wawili wanakuja mbele yake,mmoja alimtambua alikuwa Issa ameshikiliwa vizuri.
“Mimi ndio Mzee Mrema,kijana huyu hapa.Alinipa shida kidogo”
Mzee Mrema akaanza kujiongelesha baada ya kuhakikisha kwamba muhindi ndiye huyo aliyekuwa anazungumza naye simuni,niya na madhumuni yake ilikuwa ni kumkabidhi nayeye apewe milioni kumi na tano aondoke zake,kabla ya kupewa pesa alianza kuwaza akipiga hesabu ni kitu gani azifanyie.Moyo wake ulikuwa ukipiga kwa nguvu sababu na umri wake wote hakuwahi kumiliki pesa kama hizo.Badala ya Mzee Kapoor kumuangalia Mzee Mrema aliyekuwa anajichekesha yeye alikuwa akimkata jicho kali Issa anavuja damu puani,hasira alizokuwa nazo zilizidi kipimo.Alitamani achomoe bastola amfyatue ya kichwa hapohapo.Hakutaka tena kuwatuma vijana wake ama mtu yoyote yule,zoezi la kutaka kumuuwa Issa alitaka kulifanya kwa mikono yake mwenyewe.
“Mzee,Kijana huyu hapa”
Mzee Mrema akaongea tena lakini kwa hofu sababu sura ya Mzee Kapoor ilimtisha kupita kiasi.
“Nipigie simu kesho asubuhi”
Mzee Kapoor akazungumza.
“Lakini Mzee wangu ime….”
“Pigia mimi asubuhi,kadi yangu hii hapa.Cheka pakia hii kwenye gari”
Kauli hiyo alipewa kijana mwingine mwenye mwili mkubwa kama Mike Tyson huyu ndiye alikuwa pembeni ya Mzee Kapoor,Issa akashikwa shati na wote wakaingia siti za nyuma.Gia ikapigwa gari ikazunguka kwa kasi ya ajabu.Kwa mara nyingine Issa alikuwa ameingia kwenye matatizo,kwa picha iliyotokea hakuwa ana uhakika wa kupona siku hiyo na alishakata tamaa ya kuishi.Mapigo yake ya moyo yalikuwa yakipiga kwa nguvu na alihofia kupita kiasi haswa alivyokumbuka mateso aliyopitia,wakati mwingine alijilaumu ni kiherehere gani kilimtuma atoke usiku wa manane,akiamini kwamba bila kufanya hivyo wenda asingekuwa kwenye matatizo.Jinsi gari lilivyokuwa linatembea kwa kasi ilimtisha mno,mbali na hapo hakuna hata mtu mmoja aliyekuwa anazungumza chochote.Badala ya gari kunyoosha Aghakhan Mzee Kapooor akakunja kona ya kushoto, akaanza kuitafuta Mabibo,akapita mahakama ya ndizi alivyofika Mabibo mwisho akalala kushoto,akanyoosha moja kwa moja, safari yake ilikuwa afike Round about ya Kigogo kwenye bonde la Mikumi,hapo ndipo pangekuwa kaburi la Issa amuuwe na kumtupa mtaroni.Hayo ndiyo yalikuwa mawazo ya Mzee huyu gaidi.Ulikuwa ni usiku mnene gari aina ya Marcedez Benz nyeusi ikapiga breki darajani, Mzee Kapoor akashuka na kuuendea mlango wa nyuma.
“Shuka,hapa ndio mwisho wako”
Mzee Kapoor akasema na alikuwa na bastola mkononi mwake.
“Shukaaa”
Issa akawa kama mwanakondoo kwa hofu na uwoga akateremka ndani ya gari akawekewa bastola na kuamriwa asonge mbele, ambapo nyuma yake alifuata Cheka mpaka mabondeni wanapolima mchicha na matembele,Issa akasimamishwa.
“Katrina amekufa,kwasababu yako.Mshenziii.Siwezi kukuacha uwe hai hata siku moja.Pumbavu”Mzee Kapoor akafoka kwa hasira na jazba nyingi.
Haikuwa utani hata kidogo,Bastola ilikuwa kichwani mwa Issa na endapo risasi ingechomoka basi ndiyo ungekuwa mwisho wake na alisikitika sana kusikia Katrina amekufa,taratibu alifumba macho yake akimuomba Mungu aipokee roho yake ahera sababu alijuwa kifo ni halali yake,hata hivyo aliona sawa kutangulia sababu aliamini kuwa mwisho wa siku kila mtu ataonja umauti.Kwa mambo yalivyoenda na jinsi Issa alivyomsumbua haikuwa rahisi kurudisha moyo wake nyuma,Mzee Kapoor ni wazi kuwa alishawahi kuuwa lakini sio kwa staili hiyo ya kumpiga mtu risasi hata yeye alijisikia vibaya lakini hakuwa na jinsi ilikuwa ni lazima ampige risasi kisha amtupe kwenye mtaro wa maji.Akaiweka bastola sawa kabisa na kuingiza kidole chake kwenye triga na kuanza kuivuta taratibu.
“Paaaaaaaaaaa”
Mlio wa risasi ukasikika kwa nguvu,damu zikaruka na kutapakaa.
***************
Kulikuwa kama kuna mtu ndani ya moyo wake anaukamua kwa nguvu,hiyo ilimfanya amwage machozi kama mtoto mdogo.Hakuwahi kuwa na uchungu wa namna hiyo,bado picha ya mkewe ilimpitia kichwani akamuona jinsi alivyolazwa miguu yake imetanuliwa huku na kule anafanya ngono na Amadour na mchezo ulivyoenda alijuwa fika kama isingekuwa rafiki yake Captain Ladislaus wenda angenyongwa kwa kosa la kusingiziwa kwa kukutwa na madawa ya kulevya.Hayo tu yalitosha kumuhukumu Marietha moja kwa moja kuwa ni msaliti na hakuelewa kama atamsamehe maishani mwake,ni wazi kwamba ilikuwa vigumu kumuacha kutokana na ndoa aliyofunga Kanisani.Wakristo hawakuwa na kitu talaka na walikuwa wanaoa mara moja,siku zote ingebaki kuwa Marietha ni mke wake tu na hakuna mtu yoyote angeweza kubadilisha hilo labda kifo tu.
Alivyowaza hayo ndipo alipochoka zaidi,mkononi alikuwa amemshika mtoto wake Abraham,Taxi aliyopanda ikazidi kusonga mbele inaelekea uwanja wa ndege,ili akwae pipa arudi nchini Tanzania.Kumuacha Marietha aliamini kabisa katika maisha yake kuna kitu kikubwa kingekosekana nayo ni furaha!Haikuwa uwongo,Deo alimpenda sana Marietha kuliko mwanamke yoyote yule ndiyo maana akatenga pesa nyingi kupanda naye ndege mpaka ufaransa ili wafurahie maisha yao ya ndoa na mtoto wao mdogo lakini badala yake alimuumiza moyo.
Taxi ilipita magorofa ya Univesel ikazidi kusonga mbele,Deo hakuelewa chochote sababu alikuwa akilia machozi kama mtoto mdogo.
“Pull over”
Deo akaongea huku akifuta machozi akitumia viganja vyake vya mkono.
“Excuse me”
Dereva ilibidi ahoji,ilionekana hakuwa mwenye uhakika kama anaongeleshwa yeye ndio maana akauliza.
“Pull over,we are going back”
Deo alisema tena akimaanisha warudi walipotoka,kwa kuwa siku zote mteja ni mfalme dereva taxi akawasha endiketa na kuweka gari kando,hapo alisikiliza maelezo aliyopewa na mteja wake,akabonyeza kioo kidogo kilichokuwa mbele karibu na gia ambacho kilikuwa na ramani,akaandika sehemu anayotaka kufika,alivyomaliza zoezi hilo akaendelea na safari ambapo mbele alikunja barabara inayokwenda Parito,huko ndipo alipopata maungio ya Laineve akanyoosha moja kwa moja ili kurudi karibu na hoteli alipomchukulia mteja wake.Deo alibadili mawazo yake na kuna kitu alikipanga kichwani kwake,hakuelewa kama kingefanya kazi ama la.Mikakati aliyokuwa ameipanga Deo ilikuwa kabambe na alidhani kwa kufanya hivyo atamkomesha Marietha.
Kitu kilichomshangaza Deo ni kimoja,Marietha alikuwa palepale alipomuacha ameinama bado analia machozi,alijisikia uchungu lakini hiyo haikumfanya abadili mawazo aliyopanga.
“Stop over there”(Simama pale)
Deo akatoa maagizo tena na gari ikasimama kandokando ya mwanamke aliyekaa analia machozi.Ilibidi Deo afungue mlango.
“Marietha”Akaita.
Alikuwa chini amekaa na hakuelewa afanye kitu gani,moyo wake ulimuuma kwa kufanywa mtumwa wa ngono wa Amadour na baadaye mumewe akamfuma.Bado hakuelewa ni kitu gani akifanye ili Deo amuamini ndiyo maana akabaki eneo hilohilo akiwa analia kwa uchungu sana huku akimuomba Mungu ampitishie mbali kikombe kinachomkabili.Akiwa katikati ya dimbwi la mawazo sauti ilimshtua hakuwa ana uhakika na sauti hiyo mpaka alivyoinua shingo yake juu,akakumbana na Deo amesimama akafuta machozi harakaharaka.
“Deo nao….”
“Ingia ndani ya gari”
Alikatishwa sentensi yake,Deo aliongea na katika uso wake hakuwa anacheka macho yake yalikuwa mekundu kama mtu aliyevuta bangi mbichi.
“Ingia ndani ya gari”
Deo hakuomba hiyo ilikuwa kama amri,Marietha hakuwa na sababu ya kubaki eneo hilo sababu alichotaka yeye ni kujielezea na kuomba msamahaa hiyo ilimfanya atembee na kuingia ndani ya Taxi kisha Deo akafuata nyuma yake.
“Take us to the Airport”
Dereva akaweka gia na kuanza safari hiyo.Ndani ya gari hakukuwa na maongezi yoyote yale bali sauti ya kwikwi kutoka kwa Marietha akiwa analia machozi,Deo alilisikia hilo lakini alilichukulia jambo hilo ni kama maigizo tu.
“De..o nao..mb..a unis..”
“Sitaki kusikiliza chochote kutoka kwako,tafadhali Marietha”
“Nip..e daki..ka moja”
“Usipoteze nguvu zako wala pumzi.Nyamaza”
Deo alikuwa siriaz na aliongea maneno hayo kwa hasira za waziwazi,mpaka wanafika uwanja wa ndege wa kimataifa jiji la Paris,hakukuwa na maelewano mazuri kati ya watu hawa wawili wanandoa.Deo alimpeleka Marietha Kijeshi na wakati mwingine alitumia vitendo kuzungumza.
“De..o sijakuelewa”
“Kama hujanielewa basi”
Tayari walikuwa wamefika langoni na wamekaa juu ya benchi lakini bado hawakuwa na maelewano mazuri hata kidogo,Marietha alijitahidi kuomba radhi lakini hakupewa nafasi hiyo hata kidogo,alijisikia aibu na mkosaji mbele ya mume wake.
“Naomba mtoto nikusaidie”
Marietha alijipendekeza tena lakini badala ya Deo kumjibu alimkata jicho kali sana.Tangu Marietha aolewe na Deo ama amfahamu hakuwahi kuliona jicho kama hilo na kwa maana hiyo hilo lilikuwa jibu tosha,akainama chini kwa uwoga.Hakutaka kuongea kitu kingine chochote mpaka inafika jioni ambapo walisimama na kuanza kutembea kuingia ndani ya mlango kwa ajili ya ukaguzi wa mizigo yao,hatimaye taratibu zote zikaisha na baadaye wakaingia ndani ya ndege.
Jinsi walivyokwenda Paris na safari ya kurejea nchini Tanzania vilikuwa ni vitu tofauti yaani kinyume chake sababu hakuna hata mtu mmoja kati yao aliyekuwa mwenye furaha.Safari iliwachukuwa masaa sita angani baada ya kutua Amsterdam,Alanda na baadaye London.Hapo waliingia ndani ya shirika la ndege nyingine ya Turkish airways.Usiku mzima walikuwa safarini na ilivyofika saa nne za asubuhi,walisikia sauti kutoka kwenye spika ikitangaza kuwa tayari waliingia Uwanja wa kimataifa mwalimu Nyerere, hivyo abiria wote walihitajika kufunga mikanda yao.Jambo hilo likafanyika mara moja na ndege ikatua na kutembea kwa kasi kisha kusimama,mpaka wanafika nchini Tanzania Marietha alijitahidi kuongea lakini ikawa kama anajiongelesha mwenyewe kwani Deo hakujibu kitu chochote kile,alivyoona milango imefunguliwa akamuweka mtoto wake vizuri na kusimama,alitoa begi dogo juu sehemu maalum kisha kuanza safari akiungana na abiria wenzake,Marietha alikuwa nayeye nyuma kama mkia.Wakatoka mpaka nje na kukodi taxi moja.
“Deo,Naomba unisikilize mume wangu.Naongea kila kitu sasa hivi”
Marietha akaanza kuimbisha tena lakini hakujibiwa chochote.
“Deo,tutaishi hivi mpaka lini?”
Kichwani kwa Deo kulikuwa na mikakati mingi mno na kwa jinsi mambo yalivyoenda haikuwa rahisi kumsamehe Marietha.Picha yake akiwa uchi wa mnyama amelazwa miguu yake ipo huku na kule ilizidi kumuumiza mtima.
“Deo”
“Marietha,tueshimiane”
Deo alijibu huku sura yake ikiwa imejikunja kwa hasira.Hakuelewa amfanye nini mwanamke huyu kahaba na msaliti,taxi ilianza safari mara moja na dereva alipewa maelekezo ni wapi afike.Walivyofika Kimara mwisho,kazi ya Deo ikawa ni kusema ni wapi dereva alitakiwa aende,wakaiacha barabara ya rami na kuingia ya vumbi wakakunja kushoto na kuzidi kusonga mbele.
“Hapo kwenye hilo geti jeusi”
Deo akasema baada ya kuiona nyumba yake.Dereva akapunguza mwendo na kusimama kabisa.
“Unapokea dolla?”
Ni baada ya Deo kujisachi na kuona hana pesa za kitanzania.
“Ndio ni…”
“Nina pesa za kitanzania Deo usijali”
Marietha akadakia bado alikuwa anabembeleza akijaribu kumvuta Deo karibu.
“Ni Dolla ngapi?”
Deo akajifanya ajamsikia mkewe.
“Deo nina pesa za kitanzania,kaka ni bei?”
“Nimekuuliza ni Dolla ngapi?Mimi ndio nitakulipa”
Hiyo ilimfanya dereva abaki njia panda hakuelewa akae upande upi,ilikuwa mara ageuke huku mara kule.
“Ni shilingi elfu sitini”
Hatimaye akamjibu Marietha.
“Ni dolaa ngapi?”
Deo nayeye akaibuka na swali lilelile huku akichomoa wallet nyuma ya mfuko.
“Dolla thelathini”
“Sawa subiri nikupe”
Haikuwa utani Deo alichomoa dola kumi kumi tatu na kumkabidhi dereva taxi kumaanisha kwamba hakukuwa na haja ya Marietha kulipa,hiyo ilimuuma sana mwanamke huyu lakini alimezea na alibaki akimtizama Deo bila kusema chochote.Biko mlinzi wa getini alivyotoka alifurahi kumuona bosi wake amefika,aliwapokea mizigo na kusaidia kuingiza ndani.
Deo hakutaka kuongea chochote akaingia moja kwa moja chumbani na kumuweka mtoto kitandani kisha kujitupa kitandani,akijaribu kutafakari jinsi mambo yalivyokwenda.
“Ina maana isingekuwa Captain Ladislaus,ningekuwa tayari nimekufa.Ningeacha mali zangu zote hizi.Kwanini Marietha kanifanyia hivi?”
Mawazo yalimiminika kichwani kwa Deo kama maporomoko ya maji,bado hakutaka kuamini kama amepona na yu hai.Hazikupita hata dakika mbili Marietha akafungua mlango,akapita kitandani na kukaa kitako karibu na Deo.
“Pole na safari Mme wangu”
“Ahsante”
Aliitikia bila kumuangalia usoni.Tangia siku hiyo Deo hakumuongelesha Marietha alimnunia na hakutaka kuongea naye kabisa kama kuzungumza ilikuwa ni salamu tu basi.Marietha hakuelewa mwisho wa mambo hayo ingekuwaje sababu kila alipotaka kujielezea ilishindikana.

Siku moja usiku wa saa saba akiwa amelala alisikia muungurumo wa gari la Deo linaingia ndani na baadaye vilisikika vicheko,alitega sikio vizuri sababu alijuwa Deo hayupo peke yake.Akatulia kama dakika moja nzima,mlango wa seblen ukafunguliwa kisha wa chumbani.Marietha hakuamini macho yake,mbele yake alisimama Deo na Msichana mwingine mdogo wa makamo maji ya kunde amevalia nguo fupi,mapaja yote yapo nje.Mbaya zaidi Deo akatoa ulimi wake wakaanza kulana denda na kushikana shikana,kila kitu Marietha alikishuhudia kwa macho yake.
“Baby I love you so much”(Mpenzi nakupenda sana)
Deo alitamka maneno hayo kimahaba hakujali kama mkewe wa ndoa yupo pembeni yake mbali na hapo hakujishugulisha naye,baada ya kumuuliza msichana huyo mdogo akaendelea kumnyonya mdomo,akatumpa kitandani.
“Deoo”
Moyo wa Marietha ulijawa na wivu na aliumia kwa kiasi cha kutosha,ndiyo maana akaanza kuita na kumtingisha Deo mgongoni.
“Wewe Marietha niachie”
Deo akasema kwa hasira na kumvuta mrembo aliyekuwa naye kitandani ambaye tayari alianza kuvua nguo zake.




Kilichokuwa kinatokea mbele yake bado hakutaka kukipitisha ndani ya kichwa chake kama ni uhalisia.Sawa,Deo aliingia na mwanamke mwingine chumbani kwao kwa nia ya kufanya naye ngono lakini aliamini kwamba watasitisha lakini haikuwa hivyo kwani alimshuhudia Msichana aliyekuwa juu ya kitanda anavua nguo zake, moja baada ya nyingine.Na Deo pia hivyohivyo tena bila ya kugeuka nyuma na alijuwa fika Deo anafanya hivyo kama kulipa kisasi.Marietha alizidi kuumia moyo zaidi baada ya kumuona Mumewe tayari yupo uchi wa mnyama anaipanua miguu ya msichana huyo na kuingiza gunzi lake.Hakujali,Marietha kuwa mkewe wa ndoa alikuwa pembeni yake licha ya yote alidhamiria kufanya ngono mbele yake akiamini kwamba nayeye atamuumiza moyo,Kiuno cha Deo kilikuwa kinaenda juu na kurudi chini, tayari alikuwa katikati ya raha za ajabu mno.
“Aaaah Aahh aaaaaah De…ooo aaaaah”
Sauti ya msichana akiwa chini ilianza kutoa miguno ya kimahaba tena kwa sauti kubwa,haikufahamika kama ni raha ama anafanya kusudi lakini alifanya hivyo huku akimkwaruza Deo mgongoni.Kama uchungu aliusikia na hasira zilimpanda,Marietha alimwaga machozi na kupanda kitandani huku akimvuta Deo lakini wapi na badala yake Deo alizidisha kukizungusha kiuno chake huku akisema ‘I love you Anifa’ ilielekea ndio alikuwa anakaribia kufika mshindo na mbaya zaidi Deo hakuvaa Condom alikuwa anaenda pekupeku ama nyama kwa nyama.
“Aaaaaaaah”
Ni sauti ya Deo ndiyo iliyosikika na kutulia juu ya kifua cha Anifa kwa kama sekunde tatu nzima,sauti ya kwikwi kutoka nyuma yake ndiyo iliyomshtua.
“Anifa nakupeenda sana,wewe ni kabila gani?”
Deo akauliza,kwa sauti ya chini lakini ilimfikia Marietha aliyekuwa pembeni anamwaga machozi na kutoa kamasi bado haamini kwamba kashuhudia kitu kama hicho,hakuelewa tukio hilo alifafanishe na nini sababu halikuwa fumanizi bali ni unyama wa hali ya juu sana!Kilikuwa ni kitendo cha usaliti na unyama kwa wakati mmoja hata kama angekuwa binadamu gani asingeweza kuwa na moyo wa kuvumulia kitendo kama hicho hata siku moja ndiyo maana Marietha alilia kwa kwikwi,hakuwa ana uwezo wa kupigana, hata kama angekuwa nao asingeweza lakini alichohisi yeye ni kitu kama lidudu limemkaba kohoni kwa nguvu sana,hizo zilikuwa ni hasira zilizozidi kipimo chake.
Alimuangalia mtoto wake Abraham jinsi alivyokuwa mdogo sana.Kama ndiyo mambo yameanza mapema namna hiyo hakuelewa huko mbeleni ingekuwaje.Deo hakuwa ana habari tena na Marietha kwake yeye hilo lilikuwa kama trela picha bado halijaanza,hakutaka kutumia nguvu yoyote ile alitaka kumkomoa Marietha kwa upumbavu alioufanya kwani aliamini kwamba dawa ya jeuri ni kiburi, hakuelewa kwa kufanya hivyo ilikuwa ni sawa na kujikomoa mwenyewe kwani alishakuwa baba na hata hivyo Marietha hakufanya kwa kupenda.Yote hayo hakuyajuwa, alichofahamu yeye Marietha alitaka kumuuwa na kubaki nchini Ufaransa!
“Hivi shule unafungua lini Adela?”
Deo akauliza swali, hapo ndipo Marietha alipogundua kwamba Deo alikuwa kitandani na mwanafunzi, akaumia zaidi.
“Wiki ijayo,tunaanza moko kisha mtihani wa Taifa”
Ni kweli Adela alikuwa mwanafunzi wa kidato cha nne katika shule ya Jangwani,kumaanisha kwamba Deo alikuwa kama ‘Sugar dad’ kwake,kutokana na mambo yalivyoenda na uwezo wa Deo kifedha akajiona yeye ndio kafika tayari,kwa maana hiyo hakujali kama ana mke au la.Deo aliunganishiwa na kupigiwa pasi msichana huyo na rafiki yake aliyeitwa Kessy,hivyo ndivyo walivyofahamiana na Anifa.
“Nataka ukimaliza mtihani,twende nje ya mkoa kidogo tukale rahaaaa”
“Kweli baby?”
“Yes,kweli”
“Nitafurahi sana”
“Vaa nguo nikudrop kwenu”
“Kwahiyo silali hapa?”
Adela akauliza huku akimuangalia Marietha kwa jicho pembe.
“No,siku nyingine sio leo”
“Okay baby,nataka kujimwagia maji”
Adela akavuta kanga iliyokuwa pembeni tena ilikuwa ya Marietha akajifunga na kushuka kutoka kitandani.
Kulikuwa kuna dharau nyingi duniani za kuvumilia lakini sio hiyo kwa Marietha,haikuwezekana hata kidogo chumba chake kitumiwe hata kanga yake pia.Kama swala Marietha aliruka na kumvaa Adela,bila kuuliza chochote alimtia kibao cha mdomo, akarusha tena kofi lingine likamfikia Adela usoni.Pembeni kulikuwa na taa kubwa ya mezani bila kuuliza chochote Marietha akainyanyua.Hapo ndipo Deo akajua tayari mambo yameharibika,akatoka kitandani uchi wa mnyama,akamshika Marietha mkono.Makofi yalikuwa makali na Adela tayari alikuwa chini kashika mdomo anaona nyota.
“Mariethaaaa”
Deo akaita kwa sauti akijaribu kumtuliza Marietha,haikuwa kazi rahisi kwani Marietha alitaka kujitoa kwa Deo na kumvaa Adela.
“Marietha tuliaaa nakwambia,tuliaa Mariethaaa”
“Deo niach…ie.Huwezi kuninyan..yas..a kiasi hi…ki”
“Lak…..paaaaaa”
Deo nayeye akapokea kibao kikali kutoa kwa Marietha aliyekuwa ana hasira kama Chui aliyejeruhiwa na mkuki tumboni.
“De…o”
“Marietha tulia,nitakulabuaaa”
“Nilabue..e tu De..o.Ni..pige si ume..zoea kunipi..ga kwani itakuw..a mara ya kwan..za”
Marietha alikuwa akiongea kwa kwikwi huku akilia machozi na haikuwa kazi rahisi kumtuliza.
“Adela vaa uwende,nitakupigia simu kesho”
Kauli hiyo ilimfanya binti huyu mdogo asimame taratibu huku akimtizama Marietha,akapita nyuma ya Deo kwa uwoga,makofi aliyopigwa yalimuogopesha na isingekuwa Deo angepasuka vibaya sana kichwani kwa kupigwa na taa ya mezani hiyo ilimfanya avae nguo zake na kusahau kwamba alitaka kwenda bafuni kuoga,akafungua mlango na kuondoka zake akimuacha Deo na Mkewe wameshikana wanarushiana maneno,Marietha aliwaka kwa hasira Deo nayeye akapandisha sauti ikawa vurugu mtindo mmoja.
“Sidhani kama nitakuja kukusamehe maishani mwangu.I SWEAR labda nife.Labda nife,Marietha ulitaka kuniua!Ulitaka ninyongwe ili iweje sasa?Kwa mapenzi yote niliyokupa”
“Lak…”
“Hapana Marietha,huwezi kujitetea kwa lolote”
Deo aliongea kwa uchungu huku akipiga piga kifua chake. Ni wazi kwamba mambo yaliyotokea siku chache yalipita kichwani kwake na yalimsumbua akili,kila Marietha alivyotaka kuongea alishindwa, Deo alikuwa akiongea kwa sauti na mwishowe akaanza kumwaga machozi ya uchungu.
“De..o Mume wangu unaenda wapi?”
Marietha aliuliza baada ya kumuona Deo anavaa nguo,akabeba funguo za gari.Akafungua mlango kabla ya kutoka mkono wake ukashikwa.
“Mariethaaa niache”
“Deo siwezi”
“Niachie niondoke”
“Deo siwezi kukuachia”
Hapo ndipo nguvu ilitumika,Marietha akasukumizwa,Deo akatoka nje.Ni kweli Deo alitaka kuondoka eneo hilo haraka iwezekanavyo.
“Biko fungua geti”
Kauli hiyo alitoa Deo akimwambia mlinzi wa getini,alivyoingia ndani ya gari alilirudisha nyuma na kutoka nje ya geti.
Akanyoosha mguu na kuzidi kusonga mbele,niya yake ilikuwa ni kwenda baa huko ndipo aliamini kuwa ni sehemu sahihi kwake.Kwa kuwa ilikuwa usiku haikuwa vigumu kufika mapema sababu hakukuwa na msongamano wa magari.
Baada ya dakika kumi na mbili alikuwa shekilango akakunja kona na kunyoosha moja kwa moja,aliikumbuka baa mpya iliyofunguliwa.
“Lashaziii pale nikifika nimtafute Mushi,tunywe kidogo”
Deo alihisi kwake pombe ndio suluisho na atapunguza mawazo kwa kiasi Fulani,alivyofika Sinza Morri akapunguza mwendo na kukunja kulia,baada ya mita kama tano hivi akawa amefika.Mbele yake kulikuwa na mkusanyiko wa magari mengi sana, ilionekana sehemu hiyo ilikuwa na watu wengi mno.Haikuwa utani kwani alikosa sehemu ya kuegesha gari lake.
“Njoo upaki hukuu anco,huko kumejaa”
Alikuwa ni mlinzi,hiyo ikamfanya Deo ageuze gari na kupaki sehemu nyingine,akashuka na kuanza kutembea mpaka baa ya Lashanzi,baa ilikuwa imejaza watu sio mchezo kelele zilikuwa mtindo mmoja.
“Karibu kaka,pita kwa kule kuna siti”
Muhudumu wa baa mnene aliyevalia kimini cha rangi nyeusi alimkaribisha Deo kwa tabasamu mwanana kisha akapita mbele,hiyo ilimfanya Deo amwangalie kwa jicho la kuibia jinsi mwanamke huyo muhudumu alivyojaaliwa kwelikweli kwa nyuma,alivyopata sehemu akavuta kiti na kuketi.
“Una mwendokasi?”
“Ndio kaka”
“Nipe Mwendokasi na Bapa”
“Sawa”
Wahudumu walikuwa wanaijuwa kazi, ndani ya dakika moja meza ya Deo ilikuwa na chupa ndogo ya bia aina ya safari pamoja na chupa ya Konyagi,hapohapo akachukuwa simu yake kwa nia ya kumtafuta rafiki yake,hakuweza kukaa mwenyewe bila kampani,hata hivyo ilielekea kuna kitu alitaka kukitoa kutoka ndani ya kifua chake.
“Hallooo Mushii”
Deo akaanza kuongea baada ya simu kupokelewa.
“Yes Deo,kuna kelele hapo ulipo sikusikii vizuri”
“Upoo wapiiii?”
“Nipo Mwananyamala hapa,ndio naingia nyumbani.Sikusikiii vizuri”
“Nipo Lashazii,njoo unywe bia”
Mchaga huyu Mushi alivyosikia bia kwanza akaachia kitasa cha mlango, udenda ukamtoka lakini alishindwa kuelewa kama Deo anamtania ama la sababu Deo aliacha pombe na kuamua kuwa mchaMungu.
“Unasemaje Deo?”
“Kuna bia zako hapa,Njoo lashazii Sinza”
“Sasa hivi?”
“Ndio fanya fasta changamka”
“Poa poa ninakuja”
Baada ya kumaliza mazungumzo kwenye simu akamimina bia kwenye glasi na kuendelea kutafakari juu ya maisha yake.Ni wazi kwamba aliachana na pombe na kuamua kumpokea Yesu Kristo awe mwokozi wa maisha yake na aliyemshauri si mwingine bali ni mkewe lakini leo hii alikuwa wa kwanza kumsaliti,bado alishindwa kuelewa nini maana ya ulokole na mpaka hapo alishaanza kupata picha kuwa hakuna kitu kama hicho kama hata mkewe aliyekuwa ana kesha makanisani kila siku aliamua kumsaliti na kutaka kuumuwa iweje tena aendelee kuwa mlokole.
“Psiii psiiiiiii wewe dadaaaa,psii psiiiii”
Deo alimuita muhudumu akaongeza kinywaji kingine na hakukaa sana Mushi akawa amefika,wakasalimiana nayeye akawa ana kinywaji chake.
“Deo,vipi tena?”
Mushi alishtuka alivyomuona Deo anakunywa maji ya dhahabu yaani bia!
“Pasha pasha kwanza”
Kuanzia hapo hakukuwa na stori tena,wakawa wanakunywa pombe.
“Mushi,wewe una mke na watoto…Inshort you have a family.I’m i right?”
Deo alivyotafakari kwa kitambo kidogo akaibuka na swali,ilielekea kuna jambo alikuwa anataka kumshirikisha rafiki yake lakini akaanzia mbali kidogo.
“Yeah,you are very right”(Ndio,upo sahihi)
“Kuna mtu ananiiomba ushauri hapa,sasa naomba unisaidie nimjibu vipi.Mimi nimeshindwa kuelewa cha kumwambia”
“Sema Deo,ni kitu gani hiko?”
“Kuna rafiki yangu mmoja ameoa na ana mke na mtoto mdogo mchanga kabisa.Jamaa anampenda sana mkewe sana yaani.Juzi hivi walikuwa Ufaransa…..”
Deo alianza kuhadithia kila kitu lakini hakutaka kujulikana kama ndiye yeye anaomba ushauri alitaka kuona nini bwana Mushi angesema,akaongea kila kitu bila kuficha na mwisho akahitimisha na kusema kwamba rafiki yake anahitaji ushauri.
“Mfano wewe ungemshauri nini,ungekuwa mimi”
“Mmmmh”
Mushi akaguna kidogo.
“Ujue kitu kimoja.Ni vigumu kwa mwanamke ambaye kaolewa kufanya usaliti,hilo kwanza ujue.Kuna kitu huyo mumewe alifanya.Nawewe ungemuuliza,huyo sijui nani sijui Shedi,ungemuuliza ulishawahi kuchepuka kama alishawahi haina haja ku complain wakae chini wayamalize,na sikufichi hakuna ndoa isiyokuwa na migogoro zunguka dunia nzima.Na unajuwa mwanamke au msichana anabadilika kutokana na mazingira…”
“Mushi,sijaomba risala.Ushauri ndio unaotakiwa”
Deo alimkatisha rafiki yake ilielekea aliguswa na maneno ya Mushi,kiukweli alishawahi kulala na mwanamke mwingine tena mbaya zaidi mbele ya Marietha na akasamehewa.
“Hapana,inabidi kwanza nikuelekeze.Subirii Deo”
“Ushauri ndio nataka hapa,blaa blaa sitaki kusikia”
Deo na bwana Mushi walizidi kunywa pombe mtindo mmoja,mpaka inatimu saa tisa kila mtu alikuwa bwii!Huyu akiongea hiki yule anajibu hivi,kifupi hakukuwa na maelewano tena kila mtu alipaza sauti kubwa.
“Weweeeee Deoooooo,listen to meeeeee.Huyo jamaaa akooo sijui naniiii sijui yeye nawewe wote maboyaaa yaniii weweee,anakuomba ushauri kamaaa huo unakaa chini na kufikiria weweee ni mwanasheriaaaa.Foolish wewe,mwambie amwache huyo mwanamkeee,Malaya tu apige chiniiiiii”
“Mushiiiii,unasemaa kwaambaa….”
Deo akauliza na kucheua kidogo,Mushi akasogea karibu.
“Mwambieee amwachee mkewe,takataka tu.Malayaaa mchafu.Ananukaaaa kama kinyesiii,mpigie simu mwambiee Mushi kasema hivi,achana na huyo mwanamkeeeeee”
“Kwaahiyo amuacheeee?”
Mushi hakutoa tena ushauri wenye busara,kichwa chake kilijaa pombe nyingi kichwani.
“Mwambieee amfukuzeeee upesi sasaaa hiviiiii”
“Okeiiiii jembeeee…Leo Mariethaaaa anaenda kwaooooo”
Wazo la Mushi kwake aliliona bora kabisa,akasimama na kuyumba kidogo ilionekana alikuwa mtungi na hana nguvu,hapohapo akaanza kutembea kwa kuyumba na kupepesuka huku na kule.Akaingia chooni na kutoa haja ndogo!
“Yaani leo Mariethaaaaaa,nakufukuza.I’m sorry sir God…Namfukuza mke wanguuuu,yaaani heeee subiri nifikeee”
Deo alikuwa akiongea mwenyewe huku akiwa ameshika kirungu chake anatoa haja ndogo,alivyomaliza alifunga zipu,kwa kupepesuka akaanza kutembea kuelekea nje ambapo huko alikuwa amepaki gari yake.Akafungua mlango na kuzama ndani,kabla hajawasha Mushi akatokea.
“Sasaaa Deoooo,mbonaaa unatakaaa kuniachaaaaa?”
“Kwaaniiii Mushiiii,ngojaa nikuuulize swaliiii,tulikujaaa wote?Jibu ni nooooo,kwahiyooo kama ulivyokuja na ondokaaa hivyo hivyooooo”
“Mimiii nduguu yakooo Deo,usiniiifanyie hivyooo alafu achaa utani.Sina hataa shilingi mojaa hapa mfukoni,nidrop basiii hapo mbele bwana”
Hilo lilikuwa wazi,Mushi hakuwa hata na thumni mfukoni mwake mahesabu yake yalikuwa ni kupewa lifti na ndiyo maana alivyopigiwa simu na Deo haraka akapanda kwenye bodaboda akijuwa kuwa Deo atampa lifti.Hakuelewa kama mambo yangekuwa kama yalivyo.
“Ebwaaaana Mushiii,siooo swala languuu…Goodnight”
Kwa mara ya kwanza Bwana Mushi alidhani wenda Deo anatania na baadaye angemwambia aingie ndani ya gari,kumbe haikuwa hivyo kwani Deo alitia gari moto na kuondoka zake na jinsi alivyoliondosha gari kwa kasi kubwa ilitisha,Deo alivuta mkanda wa gari na kufunga kwenye kiti kwa usalama akakanyaga mafuta mengi na kuzidi kusonga mbele,kichwa chake kilijaa mwanamke anayeitwa Marietha na alitaka afike kwake haraka sana ili amtimue na hilo aliamini lingeenda kutokea usiku huohuo,hakutaka kujali kwamba ni usiku sana ama la!
Nusu saa badaaye alikuwa getini anapiga honi,mlinzi akakimbia na kusukuma geti.Gari likaingia ndani,Deo akashuka na kuanza kutembea kwa kuyumba.
“Weweeee Bikooo usifunge getiiiii”
Ilikuwa ni sauti ya Deo iliyojaa ulevi mkubwa.
“Bosi unatoka tena?”
Badala ya kufanya alichoambiwa Biko akauliza swali,hiyo ilimkera Deo.
“Nimekwambia usifuuuunge geeeeti.Liachee hivyo hivyoo”
“Bosi sijakusikiaa”
“Hiviiiii,wewe ni kiziwiiiii?Liacheee geti wazi”
Kwa kuyumba na kupepesuka akasukuma mlango na kuzama ndani,moja kwa moja bila kuuliza chochote akaingia chumbani.
“…..Baba wa Majeshi,ninakemea nguvu na hila zote za Shetani.Jehova naweka mikononi ndoa yangu,Jehova namuweka mikononi mwako Mume wangu.Naamini wewe ndio kimbilio la wanyonge baba wa majeshi….”
Deo alikumbana na Marietha akiwa katikati ya maombi amesimama anasali huku machozi yanamtoka na mara kadhaa alikuwa akimtaja mumewe.Jambo hilo halikumshtua Deo hata kidogo bali alilitafsiri kama unafki ama maigizo Fulani ya jukwaani.
“Weweeee kahaba mpenda wazunguuuu,nyumbaa yangu sioo kanisaaaa.Embu fungua macho nikwaambie jambo Fulani..Anyway sio nikwambieee nataka utoke sasaaa hivi kwangu”
Deo alisema lakini Marietha alizidi kuomba na kukemea,hiyo ilimfanya Deo ampige pige begani na kumvuta akimtingisha.
“Mungu hawezi kuuusikiiliza maombiii yako weweee Malaya,hivi unafikiri Mungu ni mtu wa mchezo mchezooooo”
“Deo ninasali”
Marietha akasema kwa unyonge.
“Mimi haini huusuuu saasaa ni hiviiiii,hapa kwanguuu ondoka.Sikutakiii kabisaaaaaa.Nendaaa kwa Amadour”
“Yesu wanguu”
“Yesu wakoo kafanyaaaa niniiiii?Sikiliiiza nikwambieeee,mimi sikutakiiiii.Ondokaaa ondokaaa ondokaaaaa.Nenda kwa Yesu wako,I mean Amadour.Mwanamkee malayaaa huna hata aibu”
“Deo,naomba unisikilize mume wangu ni….”
“Weeeeweee Shut up…Shiiii shiiiiiii mimi siooo mumeooo.Hiviiii mimiii niwe mumeo,mumeo nilikuwaaaa zamaniiii,sasaaa hivii wewe matawiii ya juuu bwanaaaa,vipi mzunguuu..Anajuwa kutia eeeh,vipi ulimkatikia sana.Mtamuuu eeeeeeh…”
Marietha aliogeshwa mvua ya matusi,akachambuliwa kuanzia juu mpaka chini.Deo alimtukana matusi ya nguoni ambayo hayawezi kuandikika kwenye kalamu na karatasi.
“Nachokuuombaaaa wewe uwendeee tuuuuu,Mimi sina shida naweweeeee”
Deo alizidi kuongea na kutukana matusi,hiyo ilimuuma sana Marietha na hakuweza kuvumilia alibaki akilia tu.
“Tokaaa bwanaaaaaa,hata ulie machoziii ya damuu”
Marietha alishikwa mkono na kuanza kusukumizwa kutoka nje.Mambo yakawa tayari yameharibika.Katika hali ya kushangaza na ya ghafla Deo alikanyaga maji yaliyokuwa juu ya malumalu,akateleza vibaya sana na kufikia kichwa puuu chali,hapohapo akatulia bila kuongea kitu kingine chochote.



Kulikuwa na ukimnya wa kama dakika moja nzima hivi,hiyo ilimfanya Marietha aanze kuogopa sababu Deo alikuwa chini amelala chali azungumzi kitu chochote,alijuwa kabisa kuna tatizo limetokea lakini hakutaka kulipitisha jambo hilo moja kwa moja kwenye nafsi yake,akabaki ameganda kama barafu kwa haraka hakujuwa ni kitu gani akifanye.Katika kutafakari kwake juu ya jambo gani alifanye Deo akazinduka.
“Ulidhaaaainiii nimekufaaaa???Ili ubakiii na mzunguuu.Hapaaa hafii mtuuuu”
Kumbe Deo alitulia makusudi ili atengeneze hoja nyingine ya kumtukana Marietha,alivyosimama akaibuka na matusi mengine tena kwa sauti akizunguka huku na kule akitupa tupa mikono kama wasanii wa miziki kizazi kipya,ilikuwa wazi kabisa Deo alidhamiria kumtukana mkewe na alimnywea ili ampe makavu yake,mbali na hapo alitaka atoke usiku huo huo.
“Nimekwambiaaaa tokaaaa Mariethaaa ohooooo”
Deo akasema na kuingia chumbani,hapo hakuwa ana kitu kingine zaidi ya kusagula nguo za Marietha na kuziweka ndani ya begi,hata iweje ilitakiwa Marietha afukuzwe usiku huohuo bila kujali lolote lile na hicho ndicho kilikuwa kinaenda kutokea,begi likatolewa chumbani Deo akapitiliza mpaka nje.
“Biko toa ili begiiiii njeee,Hurry up”
Mlinzi wa getini alionekana kushtuka sana na tukio hilo,haikuwezekana hata kidogo kuamini kwamba Deo anamfukuza mkewe usiku wa manane, alitamani kuingilia na kusuluisha lakini aliogopa kibarua chake kuota nyasi na ukoo mzima ulikuwa unamtegemea yeye.
“Deo nitaenda wapi usiku wote huu?”
“Usiniulizee mimiii bintiiiiii”
“Namuomba mtoto”
“Mtoto ganiii?”
“Abraham”
“Mariethaaa nitakuuuwa ujuweee,nadhani hunijuii sasa subiri hapoo uone”
Kila kitu kilishuhudiwa na Biko,mlinzi wa getini.Deo na Marietha walikuwa katikati ya uwanja na Marietha anaambiwa atoke nje ya geti wakati ulikuwa ni usiku sana jambo ambalo lingekuwa hatari mno.
“Mariethaaa tokaaaaaaaaa,Mariethaaaa ondokaaaaaaa”
Deo akawa kama anaimba yupo juu ya ngazi anahesabu vidole vyake.
“Marietha ondokaaaaa”
Baada ya kusema hivyo tu akazama ndani kama mkuki,moja kwa moja akaingia stoo na kutoa sime refu lenye makali kotekote,akatoka nalo nje.Hapo ndipo Marietha alipojua kwamba mwanaume huyo hana masihara,bila kuuliza chochote alitafuta geti lilipo na kuanza kukimbia akitoka nje,Deo hakuwahi kufanya kitu kama hicho katika maisha yake ni wazi kwamba ilionekana kama mtu aliyechanganyikiwa.
Lakini haikuwa hivyo,picha ya Marietha akiwa anafanya ngono kitandani ndiyo iliyomtia hasira na alivyochanganya na kiasi kikubwa cha pombe ndio ikawa kabisa,licha ya Marietha kukimbia Deo alikuwa nyuma yake anamkimbiza.
“Ananiuwaaaa,Ananiuwaaaa”
Marietha alipiga kelele huku akikimbia ili kuokoa uhai wake,kusimama kulimaanisha angegeuzwa kuwa bucha la nyama kwa kukatwa na panga.
“Simama malayaaa weweeee”
Kutokana na ulevi hakuwezi kukimbia mbali zaidi,akasimama.
“Ole wakooo nikushikee”
Deo alikuwa akihema kwa pupa,akageuza na kuanza safari ya kurudi nyumbani kwake,moja kwa moja akapita na kujitupa juu ya kochi, akasimama tena na kutoka nje.
“Wewee Bikooo,funga getii.Ukifunguuuua utarudi kwenuuu leoleo”
Yalikuwa ni maagizo,Deo akarudi seblen na kulala fofofo,kutokana na ulevi akapotelea kabisa usingizini.
***************

“Ng’aaaa ng’aaaaa ng’aaaa ng’aaaaaa”
Ni sauti ya mtoto mchanga ndiyo ilikuwa ikitokea chumbani kwa sauti kubwa,alikuwa ni Abraham baada ya kuzinduka kutoka usingizini asubuhi ya saa kumi na mbili, ilielekea alikuwa akitaka kunyonya.Chumbani hakukuwa na mtu yoyote yule,akazidi kupaza sauti mpaka machozi yakamkauka lakini wapi, hiyo ilifanya mpaka majirani wasikie,kutokana na kelele walizosikia usiku wa jana nakuunganisha mtoto kulia ilibidi watoke nje na kufika getini kwa Deo,walichokiona kiliwashtua,Marietha alikuwa pembeni ya geti amejiegesha ametulia,hawakuelewa kwamba amekufa au amelala.Kitu hicho kiliibua maswali mengi sana vichwani mwao.
“Yule si Marietha?”
Mwanamke mmoja mtu mzima alimuuliza mume wake aliyekuwa pembeni,hakutaka kukubaliana na swala hilo kwamba ndiye yeye Marietha.
“Mmmh”
“Mariethaa,Mariethaaa”
Marietha akajitingisha na kuangalia upande wa pili,watu aliowaona walimuogopesha haraka akafuta machozi yake na kusimama.
“Mmekuja muda mrefu hapa?”
Akajifanya kama hakuna kitu chochote kilichotokea.
“Kuna nini mbona upo nje?”
“Ninapunga upepo tu”
Alificha ukweli.
“Marietha,kweli?”
“Ndio”
“Mumeo yuko wapi?”
“Yeye,ametoka.Yupo ndani”Alibabaika.
Kuna kitu walijifunza kutoka kwa Marietha,kulikuwa kuna tatizo kubwa sana lililokuwa linamkabili jirani yao.Ni kweli,sio siri Marietha alikuwa ana matatizo makubwa pengine kuliko mwanamke yoyote yule ndani ya ndoa yake,japokuwa alikuwa mwenye matatizo lakini hakuwa tayari kuyaanika wazi kwa mtu yoyote yule.
“Mtoto mbona analia sana ndani?”
“Ndio nataka kuingia”
Marietha akaligeukia geti na kuligonga,hakuwa ana uhakika kama lingefunguliwa kutokana na mambo yaliyotokea, hiyo ilimfanya aanze kuogopa kabla ya Deo kutokea.
“Bikoo,usifungue geti nakuja kufungua mwenyewe”
Ilikuwa ni sauti ya Deo kutokea ndani,ilielekea alisikia geti linavyogongwa.Biko akarudi nyuma na kufuata kauli ya bosi wake,Deo akatembea mpaka getini na kulifungua,akakumbana na majirani akiwemo Marietha pembeni.
“Za asubuhi?”
Deo alisalimia majirani bila kumuangalia Marietha usoni.
“Salama Deo,vipi hali?”
“Nzuri”
Aliitikia kwa sura iliyojaa makunyanzi bila tabasamu,hiyo iliwafanya majirani waanze kuangaliana ilielekea kila mmoja alimtegea mwenzake aanze.
“Tumesikia mtoto analia”
“Mtoto gani?”
“Mtoto,Abraham”
“Nyie inawahusu nini?”
Deo akauliza kwa dharau,hakupenda kuingiliwa kiundani zaidi.
“Lakini sisi ni majirani”
“Ahsante”
Geti likafungwa,Deo akaingia moja kwa moja chumbani na kumbeba mtoto wake na kuanza kumpa maziwa ya kopo,alikuwa yupo tayari kuwa Mama yeye na Baba vilevile.Alivyohakikisha kila kitu kipo sawa,akaingia kujimwagia maji na kuvaa nguo zake,akambadilisha mtoto na kumvalisha mavazi safi, akamuweka begani na kubeba funguo za gari.Alivyofika nje akaingia moja kwa moja ndani ya gari,geti likafunguliwa akatoa gari nje ingawa aliwakuta bado majirani zake pamoja na Marietha nje lakini hakujishughulisha,alizidi kukanyaga mafuta na kutokomea kwenye kona,akaingia barabara ya lami.
Bila aibu yoyote ile Deo aliingia ofisini akiwa na mtoto mchanga begani kwake,wafanyakazi wake walimshangaa lakini hakuonekana kulijali hilo.
“Shikamoo bosi”
Wote wakamsalimia kwa wakati mmoja lakini hakujibu,alinyoosha mpaka ndani ya ofisi yake na kukaa kitini.Ingawa alifanya hayo yote hakuweza kubadilisha mambo yaliyotokea na hiyo ilimfanya aumie moyo kwa kiasi cha kutosha,nusu saa lizima alikaa ofisini akitafakari.Wakati mwingine alitamani siku ziende harakaharaka ili aweze kusahau lakini hilo halikuwezekana hata kidogo.Mlango uligongwa lakini kutokana na kuwa mbali kifikra hakuweza kuusikia,mpaka unafunguliwa hakusikia.
“Boss,boss!Boss”
Ni sauti ya msichana mdogo ikitokea mbele yake,hiyo ilimfanya Deo ainue shingo yake sababu hakuwahi kuisikia sauti hiyo kabla.Ni kweli,msichana aliyesimama mbele yake mnene kiasi mweupe mwenye mashavu makubwa,amevalia sketi fupi na kufanya sehemu ya mapaja yake yawe wazi alikuwa mgeni kwake.
“Wewe ndio Hannah?”
Deo akauliza huku akianza kumkagua kuanzia juu mpaka chini,alikuwa ni msichana mzuri mwenye sura ya kipole.
“Ndio,naitwa Hannah Golden Mkumba”
“Ndiyo yule wa Kampala?”
“Ndio boss”
“Hope hautoniangusha”
“Siwezi boss”
“Okay weka hayo mafaili hapo mezani”
Hannah alikuwa mfanyakazi mpya katika kampuni inayoongozwa na Deo Karekezi katika kitengo cha Manunuzi,alikuwa ni binti mdogo kati ya umri wa miaka 22-25 hivi,kipindi anafanyiwa usaili Deo alikuwa nchini Ufaransa lakini habari hizo alikuwa nazo sababu kila kilichoendelea katika kampuni yake alikuwa akitumiwa taarifa,kwa Deo na Hannah hiyo ndiyo ilikuwa mara yao ya kwanza kuonana ana kwa ana.Ndiyo maana hata Hannah akaanza kuhaha sababu ilikuwa mara yake ya kwanza kuonana na tajiri yake tangu apate ajira.
“Hannah”
Deo akaita baada ya kumuona anaukaribia mlango,sio siri Hannah alijaliwa kupewa makalio makubwa na alivyokuwa anatembea alitingishika kwa nyuma ingawa Deo hakuwahi kutamani lakini siku hiyo alijishangaa,msichana huyo aliteka hisia zake ghafla.
“Abee boss”
“Mwambie Dora aniletee kahawa”
“Sawa bosi”
Hannah akageuka hakuelewa alikuwa anamnyanyasa bosi wake kwa kiasi cha kutosha.

************
Mapendo na mapenzi yote badala ya kuwa kwa Marietha sasa yalihamia kwa mwanaye Abraham,kwa wakati huo aliamini Abraham ndio kila kitu na tayari alishaanza kumuandikisha mali zote.Baadaye akauza gari aliyomnunulia Marietha na kununua gari nyingine ndogo hiyo aliandika jina la mwanaye Abraham Deo Karekezi,na baadhi ya hati za nyumba pamoja na viwanja vyote alivyokuwa navyo vilikuwa mali ya Abraham,aliamini siku yoyote akidondoka na kuaga dunia Marietha atachukuwa mali na kumtesa mwanae,hakutaka hilo litokee kabisa.
“Sasa hapa hata nikifa siku yoyote Abraham,vitu vyote hivi vyako.Sawa mwanangu”
Siku hiyo Deo alikuwa anaendesha gari pembeni ya kiti kamuweka mtoto wake,ilikuwa ni jioni ya saa kumi na mbili,alivyoingiza gari ndani alikumbana na magari mengine matatu,mawili aliyajuwa lakini lingine lilikuwa ngeni kwake,walikuwa ni wageni kutoka kanisani hilo alilijuwa wazi.Akashuka ndani ya gari na Abraham,wakaingia mpaka seblen huko alikumbana na umati mkubwa kutoka kanisani na katikati yao alikuwa Marietha ameshika Biblia,alipopagawa zaidi kushoto alimuona Leila mwanamke anayemchukia kuliko kifo,hilo ndilo lilimfanya akasirike zaidi.
“Bwana asifiwe”
Ni Muumini mmoja wapo ndiye aliyetoa salamu alivyomuona Deo.
“Nawasikiliza”
Badala ya kujibu swali,akataka kujuwa nini maana ya ugeni huo wa kushtukiza.
“Deo,kaa chini tuzungumze”
Hapo Deo hakuwa na kipingamizi,akatembea mpaka kwenye sofa na kuketi akitaka kusubiri ni mbinu gani wazee hawa wa kanisa wangetumia kumshawishi licha ya kukaa lakini aliamini kwamba hatoweza kumsamehe Marietha habadani sababu alijuwa fika kinachotaka kuongelewa.
“Marietha simama”
Mmoja wapo akasema kisha Marietha kusimama katikati ya watu waliomzunguka,akamtizama kila mtu kwa zamu kisha macho yakagongana na Deo.
“Hakuna mtu yoyote anayejuwa ni kitu gani nilikifanya.Ni aibu kubwa sana lakini sina jinsi,nina mpenda Mume wangu na nitampenda siku zote za maisha yangu.Leo hii naamua kusema ukweli mbele yenu……Nilisafiri na Mume wangu mpaka nchini Ufaran..sa”
Marietha alianza kusimulia kila kitu,na katika historia yake hakuacha neno lolote lile nyuma.
Alieleza jinsi Amadour alivyomlaghai na kumtumia akawa mtumwa wake wa ngono ili Deo awe huru,alivyofika hapo akaanza kumwaga machozi ya kwikwi.Kila mtu aliguswa na simulizi hiyo,Deo ndio usiseme!Moyo wake ulimuuma ajabu na alianza kujilaumu kwa kumtuhumu Marietha moja kwa moja bila kumsikiliza,bila kutegemea alijikuta nayeye anamwaga chozi,akainama chini kidogo na kutoa kitambaa,akajiziba usoni.Hakutaka mtu yoyote yule ajuwe kama analia.
“Ni..po hap…a Mbe..le Mume wang..u Deo.Naj..ua nimekosea kwasababu naku..penda sikutaka ufu..ngwe sikuele...wa Deo.Nakupenda Mume wa..ngu”
Marietha alianguka kwa magoti akamsogelea Deo alipo huku akilia machozi akisema kwamba asemehewe.Hiyo ilimfanya Deo azidi kulia tena na tena,akamuweka Abraham kando na kusimama,akamshika Marietha mikono na kumnyanyua.
“Si…mama mke wangu..NIMEKUSAMEHE NAKUPEN..NDA SANA”
Maneno hayo yalimtoka Deo akiwa analia,akamkumbatia Marietha.Waumini waliokuwa pembeni wote waliinua mikono yao juu kwa furaha,wakimshukuru Mungu!




Kwa moyo mmoja na mkunjufu Deo aliamua kumsamehee mke wake wa ndoa,hata hivyo alijilaumu sana kwanini hakumpa muda wa kujielezea,hakutaka tena vitu vilivyopita viisumbue akili yake kwani ilikuwa ni lazima siku moja vije kuwa historia ili maisha yaendelee kama kawaida kwani aliamini Marietha ndiye mke aliyepewa na Mungu,aliyachukulia mambo yaliyopita kama changamoto na majaribu tu,ndiyo maana mikono yake akaizungusha mngongoni kwa Marietha na kumkumbatia huku akilia machozi ya uchungu,akiomba asamehewe.
“Huja..nikosea Mume wangu”
Marietha alijibu bado akiwa na kwikwi kohoni, ilionekana hata yeye bado hakuamini kama Deo kamsamehe, shukrani zake zote alimpa Mungu wake aliye juu mbinguni asiyeshindwa na jambo lolote lile.Waumini kutoka kanisa la Jehova Elishadai walipiga makofi na kuanza kuimba nyimbo za kuabudu na kumsifu Mungu maana kwao jambo hilo walilipitisha moja kwa moja kama ni muujiza kutoka kwa Mungu,baada ya kila kitu kufanyika wakapiga ibada na wote kufurahi.
Ikawa kama mchezo wa kuigiza vile Deo kumsamehe Marietha kumbe ndio kweli,wageni walivyoondoka Deo alimsogelea mkewe na kuzidi kumuomba msamahaa ingawa hakujua kwanini.Furaha ikarudi upya ndani ya familia mambo yakawa shwari, wakaendelea kumlea mtoto wao Abraham kwa mapenzi yote,siku hiyo usiku walivyomaliza kula na kusali kisha kumlaza Abraham waliingia chumbani kama wafanyavyo wanandoa na kuanza kupiga stori za hapa na pale huku wakicheka,hakika kila mtu alikuwa mwenye furaha moyoni mwake.
“Love”
Deo akamuita mkewe kimahaba.
“Abee”
“Hivi unajuwa nakupenda sana”
“Ndio najuwa”
“Umejuaje?”
“Huwa unaniambia kila siku”
Marietha alikuwa ndani ya mtandio mmoja peke yake,nusu ya mwili wake upo wazi na alikuwa amelala kihasara hasara,hiyo ilimfanya Deo asisimke kwa kiasi cha kutosha.Uzuri na mapaja ya mkewe yaliyokuwa na supu nyingi vilifanya damu yake itembee kwa kasi kubwa sana,hakuwa na haja ya kuuliza kitu gani akifanye, alichofanya ni kumsogelea mkewe na kumpa mdomo ambapo hapo alitoa ulimi,Marietha akaupokea wakaanza kubadilishana mate kwa staili ya kunyonyana ndimi.Mkuki wa Deo ulikuwa umesimama tayari ingawa ulikuwa ndani ya boxa,Marietha aliliona hilo kama mke alitakiwa kulifanyia kazi mara moja swala hilo na likaisha, hapo ndipo alipotoa boxa ya Deo na kuanza kuuchuwa muogo wa jang’ombe.Marietha hakuishia hapo,alichofanya ni kuweka mtandio wake kando ya kitanda akamsogelea Deo karibu na masikio na kupenyeza ncha ya ulimi wake.Jinsi alivyofanyiwa na Marietha ilikithiri,hiyo ikafanya mpaka ahisi damu yake imesimama akajiona yupo juu angani vitu vyote anaviangalia kwa chini,Deo alihisi raha ambazo hazikuweza kuelezeka.Kuna kama vitu alivihisi vinamtekenya kutokea miguuni na kupanda taratibu mpaka juu.
“Aaaaaah”
Hiyo ilikuwa sauti ya Deo huku akijinyonga nyonga,ukweli ni kwamba kuna vitu ndani ya damu yake alivihisi vinakuja kwa kasi ya umeme.Akamvuta mkewe mdomoni na kuanza kumnyonya mdomo kwa fujo,Marietha alivyoona hali hiyo alijuwa nini maana yake,akazidi kuuchuwa mkungu wa ndizi mpaka risasi nyeupe nzito zikaruka kwa kasi na kumchafua vibaya sana usoni na kifuani,hapohapo Deo akatulia,hayo ndiyo yalikuwa mahesabu ya Marietha kumfanya Deo afike mshindo kabla ya mechi kuanza.
“Pole baby”
Marietha akasema huku akimpangusa mumewe kwa mtandio kisha nayeye akajipangusa na kumlalia kifuani.
“Nakupenda sana Deo wangu”
“Hata mimi,tena zaidi yako”
“Kweli?”
“Niamini nayosema”
“Nakuamini sana,alafu baby”
“Yes”
“Lakini basi…”
“Ulitaka useme nini?”
“Sio kitu Darling,nakupenda”
“Ahsante love,nakupenda pia”
Kuanzia hapo zilifuata stori za Mahaba,Marietha alielezea juu ya hisia zake na Deo akasema jinsi gani anavyompenda Mkewe kifupi kila mtu alimwaga kile kilichokuwa ndani ya moyo wake ingawa walipitia mambo mengi nyuma lakini waliyachukulia ni kama mitihani tu na waliamini kwamba bado kuna milima na mabonde mengi hivyo wanatakiwa kuwa imara na kushikana kwa pamoja.
“Baby twende tukaoge,alafu nataka kubadili shuka”
Marietha akasimama kisha Deo akafuata na kuingia bafuni,bomba la mvua likafunguliwa na maji kuanza kutokea kwa juu,Marietha siku hiyo alikuwa kama kachanjiwa vile maana alikuwa ana moto kwelikweli, bila kupoteza wakati akaanza uchokozi kwa kushika ndizi ya Deo taratibu akiwa anaichua huku akikilamba kifua chake,gari la Deo taratibu likaanza kuwaka kwa mbali,taratibu mishipa ya mnara ikaanza kujitokeza na ukaanza kukakamaa na kuwa mgumu,Marietha akajuwa tayari gari limewaka na ni lazima aliendeshe,maji yakiwa yanamwagika kama mvua akamvuta Deo midomoni mwake wakaanza kulana denda kwa fujo.Safari hii Deo hakutaka kuwa mzembe kiasi hicho ilikuwa ni lazima nayeye ajiongeze ndiyo maana akapitisha mkono wake mmoja kwa chini karibu kabisa na ikulu ya Marietha akitumia kidole cha kati,hapo alikumbana na kinyama kidogo na laini mithili ya kiharage,akaanza kukipekechua taratibu,akateremsha ulimi wake mpaka juu ya chuchu za Marietha,hapo ndipo mwanamke huyu akawa hajiwezi tena,akawa kama amepoteza fahamu kabisa akayafumba macho yake alichokuwa anahisi hakikuwa kitu cha kawaida,akaushika mnara wa Deo uliokuwa wima kama msumari wa nchi saba,mwenyewe akainua mguu wake mmoja juu na kutumbukiza ndizi ndani ya mgodi wake, ni wazi kwamba alikuwa amezidiwa na hakutaka kupoteza muda.
“Deeee….o”
Marietha aliita huku akiwa amefumba macho yake,hajiwezi tena.
“Mmmmh”
Deo akaitikia kwa kuguna huku akiwa anaseti mitambo,akauweka mguu wa Marietha vizuri na kutumbukiza ndizi mpaka ndani ambapo alihisi kuna majimaji tayari na joto lenye nyuzi centigredi 17.
“Nakuupenda Deooo,usiniiiache mumeee wanguuu”
Hayo yote yalikuwa yanamtoka Marietha,Deo akaona isiwe tabu kwanini waendelee kujitesa bafuni wakati wana chumba chenye kitanda cha sita kwa sita,akauchukuwa mguu mwingine wa Marietha na kumbeba juu juu,wakaingia chumbani.Kabla ya kufika akamuweka ukutani.Marietha akawa anaelea juu juu,huku chini Deo anazungusha kiuno chake taratibu,alimpenyeza nyoka wake katika kila pembe ya mgodi.Alivyoona haitoshi akambwaga kitandani puuu,akapanda juu yake na shughuli kuanza upya,kutokana na kufunga bao la kwanza tayari,ilikuwa vigumu kwake kufika mshindo hiyo ikafanya Marietha afike mlima kitonga Mara mbili na alikuwa hoi,yupo chini ya Deo mguu wake mmoja upo begani kwa Deo,ndizi ipo ndani ya mgodi wake.Alivyoona Deo anazidisha kasi na kumsogelea mdomoni akajuwa tayari anakaribia kufika,alichofanya yeye ni kumpa ushirikiano kwa kuanza kukinyonga kiuno chake.
“Aaaaaaaaaaaaaaaah”
Deo hapohapo akatulia kifuani kwa Marietha huku majasho yakiwa yanatoka kwa mbali.Baada ya kufanya tendo hilo la ndoa lililohalalishwa,wak­aingia bafuni na kujimwagia maji,shuka likabadilishwa na kila mtu akajitupa kitandani kulala.

***********

Ndani ya mwezi mmoja Deo alinawiri na kuzidi kuwa ‘handsome’akapata kitambi kiasi,ngozi yake ikawa laini mno na muda wote alikuwa mwenye furaha kwa kiasi cha kutosha,nyuma ya yote hayo alikuwa amesimama mkewe Marietha kwa kuhakikisha kwamba Deo anakula vizuri na milo yote yenye vitamin na kumpa furaha.Na ilikuwa wazi kila mwanamke alitamani awe Marietha,hata hivyo na wengine walidiriki kujitoa kimasomaso kumtongoza na kumwambia kwamba wanamtaka kimapenzi na siku zote jibu lake lilikuwa ‘NO NINA MKE’hakuna hata mwanamke mmoja kati yao aliweza kumnasa ingawa walitumia mitego mingi lakini Deo aliwa ‘shit’ sababu akili yake yote ilikuwa kwenye familia yake na alifanya kazi kwa bidii na kukusanya pesa kwa ajili ya Abraham baadaye.
Abraham alizidi kukuwa na kunawiri,alikuwa ni mtoto mzuri pengine kuliko yoyote yule,kila mtu alitamani kumbeba mtoto huyo na iwapo siku angetokea angevalishwa sketi ungesema ni mtoto wa kike,wazazi wake walikuwa weupe!Hiyo ilifanya awe mwenye rangi nyeupe zaidi akafanana na shombeshombe,sura akachukuwa kwa mama yake.
“Mtoto wako mzuri Marietha,khaaaa”
Hizo ndizo sifa walizokuwa wanamwaga majirani.Kuna kipindi meneja wa kampuni ya mafuta ya ‘babycare’alimfuata Deo na kumuomba Abraham afanye tangazo,hakukuwa na shida.Abraham akachukuliwa kwa ajili ya picha za matangazo na sura yake ikawa kwenye mafuta ya kopo.Deo na Marietha wakalipwa mamilioni ya pesa ikawa furaha kubwa sana kwao.
Kuna kitu ambacho Deo alikisoma usoni kwa Marietha kadri siku zilivyokwenda mbele,Marietha alipunguza furaha yake,hakuwa kama mwanzoni ilibidi suku hiyo Deo alivyorudi kutoka kazini amuulize mkewe,hakutaka kukwepesha swali.
“Una nini mke wangu?”
Deo akamuuliza mkewe!
“Hapana nipo sawa Deo”
“Marietha,mimi nakujuwa huu mwaka wa sita.Najuwa ukiwa na furaha nakujuwa ukiwa na matatizo nakujuwa ukiwa katika hali yoyote ile,niambie nini tatizo mke wangu,mimi ndio mwandani wako”
“Deo….”
Marietha akaita, ilionekana kuna kitu alitaka kuzungumza lakini akaupiga mdomo wake ‘stop’
“Naaam”
“Niko sawa”
“Marietha wewe ni mtu wa Mungu,kuficha hivyo unakuwa unafanya dhambi kubwa na unaidanganya nafsi yako”
“Deo niko sawa mume wangu,ngoja nikupakulie chakula ule”
“Abraham yuko wapi?”
“Amelala,alafu alikusubiri kweli”
“Kamwamshe”
“No Deo,amelala mwache apumzike”
Hapo hakukuwa na namna nyingine ya kumfanya Deo atake kumuamsha mtoto wake,akala na kusimama tayari kwenda kulala huku nyuma akimuacha Marietha ameshika mikono shavuni yaani tama,ni kweli alikuwa ana mawazo kuliko kawaida na alihitaji ushauri wa juu ya kitu gani akifanye sababu aliogopa akimueleza Deo yangeibuka mambo mengine,kwa maana hiyo hakutaka kufanya hivyo alichofanya ni kufuta meza na kutoa vyombo,akaingia jikoni na kuviosha,akaacha kila kitu katika hali ya usafi kisha kuingia chumbani huko alimkuta Deo tayari ameuchapa usingizi.
***********
“Una mimba?Sasa si umwambie Mumeo,kwanini unaniambia mimi?”
“Ndio ninaweza kumwambia lakini nina wasiwasi sio ya Deo”
“Una maanisha nini?Marietha niambie ukweli”
“Nahisi ni ya yule mzungu”
“Mzungu gani?”
“Kule ufaransa,nilivyoenda na Deo”
“Mungu wangu”
Ni wazi kwamba Marietha alikuwa mjamzito na aliamini mimba hiyo ilikuwa ya Amadour kwa asilimia themanini sababu walifanya ngono kavukavu,ndiyo maana alikuwa ana mawazo chungumzima, hakuelewa siku hiyo akijifungua itakuwaje,Deo atasema nini.Ni wazi kwamba ndio ungekuwa mwisho wake na Deo.Hiyo ilimfanya hata Tujaely Mzava aweke mkono wake mdomoni,jambo hilo hata yeye aliliogopa kupita kiasi.
“Ndio hivyo Tuja,sijui nifanye nini”
“Wewe una uhakika hiyo mimba sio ya Deo?”
“Ndio,nina mashaka hayo.Nataka kuitoa bora iwe hivyo”
“Noooo,usifanye hivyo ni dhambi kubwa, sasa mfano kama niya Deo?”
Tujaely Mzava alijaribu kutoa ushauri wake ili kumtuliza Marietha aliyeonekana mwenye ‘stress’nyingi kuliko kawaida.
“Eh Mungu,kwanini mimi?”
Marietha alisema kwa unyonge.
“Marietha sikiliza,mwambie Deo”
“Nimwambie nini?”
“Kwamba wewe ni mjamzito”
“Alafu?”
“Tutaanzia hapo”
“Hapana,mimi namjua Deo.Ataniua”
“Sasa atakuuwa vipi?”
“Akijua sio yake”
“Wewe una uhakika gani sio yake”
“Tuja,nipo njiapanda sijui cha kufanya”
Marietha alikuwa amevurugwa kuliko kawaida na alihitaji ushauri wenye busara sana.


Mawazo ya kwamba mtoto aliyebeba tumboni mwake inawezekana akawa wa Amadour ndiyo ilifanya mpaka afunge safari na kwenda Mbezi beach kuonana na rafiki yake Tujaely Mzava,akiamini kwamba atapata ushauri ama kitu gani akifanye,ni kweli alipewa ushauri mzuri lakini kwake bado aliendelea kudhani hivyohivyo,akapiga picha siku atakapojifungua mtoto ndugu jamaa na marafiki wapo wodini wanamtizama kisha baadaye wanaoneshwa mtoto wa kizungu,ingekuwa aibu kubwa kuanzia kwake familia yake na pia angekuwa amemuaibisha mumewe Deo Karekezi,licha ya kumuaibisha tu,ndoa yake ingekuwa na doa kubwa lisiloweza kufutika hata iweje,hilo ndilo lilimuumiza zaidi moyoni.Alimuangalia Tujaely kwa macho yaliyojaa kitu fulani.
“Tuja,nitaitoa hii mimba”
“Marietha usije ukajaribu kutoa mimba,ni dhambi kubwa sana.Na umwambie Deo”
“Nitajaribu kufikiria,wacha niwahi nimemuacha Abraham mwenyewe nyumbani”
Marietha aliaga na kutoka nje ambapo alikuwa amepaki gari aliyokuja nayo,akaingia ndani na kuegemea usukani.Picha akiwa nchini ufaransa na Amador kitandani ikampitia ghafla,kwa kitendo hiko ilifanya ajichukie na kumlaumu Mungu wake kwa kuruhusu jambo hilo litokee,machozi yakaanza kumlenga na kushika tumbo lake.Pepo baya ghafla likamvaa na kumtuma amtoe mtoto haraka iwezekanavyo yaani ameze vidonge na kumuuwa ama njia yoyote ile ilimradi tu mimba itoke.
“No nooo”Alikema.
Marietha aliwasha gari na kukanyaga mafuta mengi,gari ikazunguka na kutimua mchanga, hakuelewa kwamba huko nje alifanya watu wapaliwe na vumbi kwa kuwa alikuwa ndani ya vioo hakuona,akazidi kusonga mbele,breki ya kwanza ilikuwa ni nyumbani kwake ambapo alimkuta Abraham bado amelala fofofo,akaingia bafuni kujimwagia maji,alivyotoka aliketi kitandani akijaribu kutafakari ni kitu gani akifanye,bado alikuwa ‘dillema’yaani njia panda.Akili yake ilivyotulia alimkumbuka rafiki yake mwingine wa karibu aliyeitwa Avin David Isame mke wa Yona Isame huyu alimjulia kupitia Deo lakini walitokea kuwa marafiki wakubwa sana,hakutaka kupoteza muda!Akatembea mpaka juu ya meza na kuchukua simu yake,hapohapo akaanza kutafuta orodha ya majina mpaka alipolifikia jina Mrs. Isame,akaruka hewani.
“Halloo”
Upande wa pili wa simu ulisikika Avin David alikuwa kwenye laini tayari.
“Avin,Marietha naongea”
“Najuwa Marietha,namba yako ninayo.Za kunitupa?”
“Siwezi kufanya hivyo ila ni majukumu tu ya kulea na mambo mengine ya kimaisha”
“Umerudi lini?Maana mara ya mwisho tulikuwa tunachat upo Paris”
“Aaah nina muda kidogo”
“Umeniletea zawadi gani?”
“Usijali kuhusu hilo,upo wapi kwanza?”
“Nipo Kariakoo”
“Kwenye lile duka lako?”
“Ndio”
“Hivi una zile perfume zinaitwa Dolby?”
“Zile zimeniishia lakini nadhani next week nikienda Dubai kupakuwa mzigo mwingine nitakuja nazo”
“Una perfume gani nzuri?”
“Ushawahi kutumia esimiaki au Ecko?”
“Nataka mbili,yangu na Deo”
“Sawa njoo dukani”
“Okay nakuja”
Kilichotaka kumtoa nyumbani mpaka katikati ya jiji kumfuata Avin David Isame sio kununua unyunyu bali mahesabu yake yalikuwa ni mengine kabisa,alitaka akae na Avin ili apewe ushauri wa jambo linalomkabili.Harakaharaka akajiandaa na kubeba kiasi kidogo cha pesa,akamchukuwa mwanaye ambaye tayari alikuwa macho.Wakaingia ndani ya gari na safari ya kwenda Kariakoo kuanza hapohapo,ilimchukuwa dakika hamsini na saba hivi kutoka Kimara mpaka Kariakoo lakini kwa kupitia njia ya jangwani na kuibukia club ya Yanga,kilichomsumbua ni sehemu ya kuegesha gari lake,Kariakoo kulikuwa na msongamano mkubwa wa magari,hiyo ilimchukuwa dakika nyingine kumi na tano ndiyo akashuka na Abraham kutoka ndani ya gari,kipima joto mkononi!Wakatembea mpaka upande wa pili ambapo mtaa mzima kulikuwa na maduka ya vipodozi na Parfume,akakunja kushoto na kusimama kwenye duka la tatu.
“Aviiiin”
Marietha akaita akiwa tayari yupo dukani kwa rafiki yake,Avin akageuka.Alikuwa ni msichana mwenye mwili mdogo lakini mwenye mafanikio makubwa kiuchumi, yeye na mume wake walikuwa wajasiliamali na hawakuridhika hata kidogo,wakafungua maduka mengine huko Kariakoo ya vipodozi vya kike na lingine la Perfume na ndiyo maana Deo Karekezi na Mume wa Avin walikuwa ni marafiki wakubwa hapo ndipo wake zao walijuana kupitia wao.
“Marietha,ndio wewe kweli?Umenenepa”
Avin akasema huku akitabasamu,haikuwa utani Marietha alikuwa amenawiri kiasi, ungemuangalia kwa nje ungesema kwamba mwanamke huyu hana shida hata kidogo kumbe haikuwa hivyo,Marietha alikuwa ameandamwa na matatizo kupita kiasi!
“Ndio mimi,biashara zinaendaje?”
“Hivyo hivyo,tunabangaiza.Pita ndani njoo ukae hapa kwenye kiti,Abraham ndio amekuwa kiasi hicho,kweli umejuwa kukuza”
Avin akaanza kuongea maneno mengi,ilionekana alikuwa mwenye furaha iliyozidi kifani sababu alikuwa mara aseme hiki mara adakie kile,stori haijaisha kashaibua hiki ilimradi vurugu mtindo mmoja.
“Kabla sijasahau,nipe perfume.Naomba Dolby na Kiss”
Avin hakuwa ana shida,akasimama na kutoa maboxi mawili ya marashi na kumkabidhi rafiki yake ambapo alilipwa pesa yake hapohapo.
“Alikuja hapa yule nanii yuleeee….Tina,unamkumbuka?”
“Tina?Tina yupi?Yule mdogo wake Amba?”
“Hapana,huyu mtoto wa shangazi yangu,unajua mpaka leo hatuongei”
“Kwanini?”
“Anakuja hapa anataka nimpe perfume bure,eti kisa ndugu yangu.Nikamwambia wewe ndugu yangu lakini kwenye biashara huo undugu pembeni.Nikamwambia hivyohivyo,ndio mpaka leo hatuongei”
“Sasa si ungempa?”
“Sasa mfano wakija hapa ndugu zangu wote kila mtu akitaka bure unadhani itakuwaje,hawa ndugu hawa ukiwaendekeza kwenye biashara wanafilisi.Potelea mbali”
Stori ziliendelea na Marietha alionekana mwenye tabasamu usoni lakini moyoni kilikuwa ni kitu tofauti kabisa,aliwaza mimba yake na hakuelewa aanzie wapi kumueleza Avin kuhusu jambo linalomtatiza mtima.
“Avin mimi nina shida kidogo”
Marietha akaanza kusema,akashusha pumzi ndefu na kumuangalia rafiki yake kipenzi usoni.
“Una shida gani?”
“Nina mimba”
“Sasa hiyo ndio shida,mimi mwenyewe nina mimba pia lakini changa ya mwezi mmoja,basi huyo Yona anasumbua,Baby umekula baby njoo ofisini,sijui baby angalia vumbi la kariakoo mara baby.Mpaka nachoka,ana wivu sio kawaida juzi alitaka kupigana na mteja hapa an…..”
“Avin”
Avin alikuwa anaongea maneno marefu,Marietha alilichukulia swala hilo kama kupotezewa wakati alichotaka yeye ni ushauri wa kitu gani akifanye sio soga ndiyo maana akawasha gari kutoka kwake mpaka Kariakoo mtaa wa chura ili ajue ni kitu gani akifanye.
“Nina matatizo makubwa sana”
“Una shida gani?”
“Nimekwambia nina Mimba”
“Sasa hapo kuna tatizo gani?”
Swali hilo kutoka kwa Avin lilimfanya Marietha aangalie chini kisha kuinua shingo juu!
“Mimba sio ya Deo”
Moyo wa Avin ukapiga paaa!Japokuwa hakuwa yeye lakini alihisi kutetemeka, alimuangalia Marietha na kusimama kisha kumuendea karibu.
“Marietha,unasemaje?”
“Mimba sio ya Deo”
“Mungu wangu,ina miezi mingapi?”
“Zaidi ya mmoja”
“Zaidi ya mmoja,miezi mingapi?”
“Kama mitatu,inakaribia mwezi wa nne huu”
“Deo anajuwa kama una mimba?”
“Hajui..”
“Mwenye mimba ni nani?”
Swali hilo lilikuwa gumu kwa Marietha kutoa jibu hakuwa tayari kusema unyama aliotendewa kwa kila mtu,hiyo ilimfanya akae kimnya kidogo.
“Mimba ya kijana mmoja hivi nilisoma naye…Avin nambie cha kufanya”
“Mmmmmh”
Avin alisikitika na alihisi kuishiwa nguvu mwili mzima,hakuelewa atoe ushauri gani kifupi alikuwa njia panda,mbali na hapo alikuwa binti mdogo tu kutoa maamuzi kama hayo mazito.
“Sasa Marietha ulikosa nini kwa Deo?Au hakurizishi vizuri”
Kama desturi za wabongo badala ya kutoa ushauri alianza kutupa lawama ambazo zisingeweza kusaidia kitu chochote kile.
“Avin,naomba niambie nifanye nini?”
“Hiyo mimba itoe,Go for abortion hilo ndilo suluisho kabla Deo hajajua.Unajuwa nini kitakupata akijua?”
“Avin,unataka niue mtoto?No siwezi kufanya hivyo”
“Sasa unataka kufanya nini?”
“Kama ya Deo sasa?”
“Wewe si umesema sijui ya huyo kijana,mbona sikuelewi”
“Asilimia themanini”
“Yaaani cha msingi hiyo mimba itoe,huo ndio ushauri wangu”
“Mimi ni mtu wa Mungu lakini”
“Ha! Haa! Haaa! Haaaaaaa!…Embu usinichekeshe Marietha Ha! Haa! Haa! ahaaaaaa.Eti mtu wa Mungu,sasa mbona umechepuka kama wewe ni mtu wa Mungu?”
Avin akamkebehi na kumdhiaki Marietha.Ushauri wa Avin kwa Marietha ulikuwa bado mgumu kidogo ndiyo maana ukatokea mzozo sababu Marietha hakuwa tayari kuuwa kiumbe kisichokuwa na hatia.
“Basi kama huwezi kutoa,sina ushauri mwingine wa kukupa”
“Avin,acha mimi niende kwanza nikajifikirie mara mbilimbili”
“Aya best,kama ukihitaji daktari mimi nitakupa”
“Okay kazi njema”
Marietha akasimama kinyonge na kumchukuwa Abraham wake,wote wakatoka nje na kuingia ndani ya gari,Avin akabaki analisindikiza gari kwa macho.
*******
Kama kawaida ya wanandoa ama wanawake siku zote,hawawezi kukaa na vitu kifuani,siku hiyo Avin akiwa na mume wake chumbani usiku,hadithi zikamuishia akaingiza habari za Marietha.
“Alikuja leo dukani pale?”
Alikuwa ni mume wake Mr.Yona Isame pia rafiki mkubwa wa Deo katika maswala ya kibiashara.
“Ndio alikuja dukani”
Avin akasema na kujiweka vizuri ili aanze kubwabwaja.
“Alikuja na Deo?”
“Alikuja mwenyewe”
“Alikuwa na mtoto wake?”
“Ndio”
“Kaja na dereva au mwenyewe?”
Mr.Isame aliuliza maswali kama polisi lakini hiyo ndiyo ilikuwa tabia yake.
“Baby nawewe umeanza maswali yako,hivi huwa unafanya makusudi au?”
“Nataka kujua Darling….Kasharudi kutoka Paris?”Akauliza tena swali.
“Hapana sasa hivi yupo Ulaya”
Avin nayeye akajibu swali lakini alikuwa katika hali ya utani.
“Baby nawewe umenishushua”
“Nawewe umezidi maswali.Nimekwambia nimemuona leo alafu unaniuliza kama karudi kutoka Paris”
“Nilikuwa sijui”
“Kuna kitu ameniomba nimshauri”
“Kitu gani hiko?”
“Ana mimba”
“Mimba?Kama wewe,ina maana mmepanga nini?”
“Akuuu”
“Sasa nini na anataka umshauri nini?”
“Anadai mimba sio ya Deo”
Ilikuwa kama Mr.Isame amesikia vibaya vile,hiyo ilimfanya akae kitako kitandani.
“Mimba sio ya Deo?!”
“Ndio”
“Mungu wangu,Deo anajuwa?”
“Hajui,hajui chochote kile.Yaani hajui kama mkewe ana mimba”
“Simu yangu iko wapi?Nataka nimpigie Deo nimueleze”
Mr.Yona Isame akasimama na kibukta chake mpaka mezani,hapohapo akachukuwa simu ili amchane Deo ukweli.



Kulikuwa kuna kama dukuduku ndani ya koromeo lake,niya yake ilikuwa ni njema kabisa kumuambia rafiki yake Deo nini kinachoendelea kuhusu mimba ya mkewe,kwa kufanya hivyo alijiona yupo sahihi na wala hakufikiria nini kingetokea baada ya kutoboa siri hiyo nzito ndiyo maana tayari alishika simu na kuanza kutafuta namba za Deo usiku huohuo bila kujali ni muda wa kupumzika.
“Griii griii”
Upande wa pili wa simu ulianza kusikika kumaanisha kwamba simu ya Deo ipo hewani.
“Yona unataka kufanya nini lakini?”
“Kumwambia Deo”
“Kumwambia nini?”
Avin alikuwa nyuma yake,hakutegemea kama mume wake atafanya kitu kama hiko.Kuambiwa kwa Deo juu ya jambo linaloendelea ingesababisha uhamasa na uadui mkubwa na Marietha kwa sababu hiyo hakutaka jambo hilo litokee kabisa,ndiyo maana akataka kumzuia mume wake asiongee chochote.
“Sasa kwanini unanizuia?Nataka nimwambie Deo,au naewewe unachepuka na usikute na hiyo mimba sio yangu”
Yona akabadili somo akimwambia mkewe sababu aliamini ule msemo kuwa Ukiona mwenzako ananyolewa zako tia maji.
“Yona achana na hiyo simu,haina haja ya kusema”
“Nitamwambia”
“Ili iweje?”
“Ili ajue,ni rafiki yangu”
“Huoni kuwa utagombanisha ndoa za watu,sasa ukimwambia alafu ikitokea mtoto ni wa Deo,hivi utaonekana vipi?”
Avin akatengeneza hoja harakaharaka ya kumfanya mumewe asipige simu,kumbe wakiwa katikati ya mazungumzo yao simu ilikuwa teyari imepokelewa na Deo na alikuwa anasikia kila kitu kilichozungumzwa.Yona akatafakari kwa muda ilielekea kuna kitu alijifunza kutoka kwa mkewe.
“Halloo Deo”
Akaweka simu sikioni ili kuanza mazungumzo na Deo.
“Mr.Yona,vipi hali?Mbona usiku usiku,unataka kunipa tenda nini?”
Deo nayeye akajifanya hajasikia chochote,alikuwa anasikilizia nini lengo la simu hiyo usiku sababu haikuwa kawaida kwa Yona kupiga simu katikati ya usiku mkubwa kama huo.
“Hapana nilikuwa nataka kukusalimia,nasikia umesharudi kutoka Paris”
“Yes nina muda kidogo”
“Mimi nakusalimia tu”
“Shukrani sana”
“Usiku mwema”
“Nawewe pia”
Simu ilimuacha Deo akiwa juu ya sofa miguu yote ipo juu anatizama luninga taarifa ya habari,kuna kitu alikisikia kutoka kwa Yona ‘Huoni kuwa utagombanisha ndoa za watu,sasa ukimwambia alafu ikitokea mtoto ni wa Deo’sentensi hiyo aliitafakari kwa upana zaidi,Abraham alikuwa pembeni chini anatambaa huku na kule,akamtizama vizuri akijaribu kulinganisha na maneno aliyosikia lakini hakupata jibu sawasawa sababu Abraham alikuwa akifanana nayeye kwa asilimia sitini hilo lilikuwa wazi kabisa na haikuwezekana hata kidogo kwamba Abraham hakuwa mtoto wake,kwa maana hiyo hakuwa ana haja yoyote ya kwenda kupima DNA.
“Tataaa taaa”
Abraham alijitahidi kuita kwa sauti ya kitoto akimaanisha Baba,hiyo ilimfanya Deo atabasamu na kutembea kisha kumbeba begani.
“Come here Son”(Njoo hapa mwanangu)
Deo alimpenda mtoto wake, ki ukweli hakuwahi kuwa na mtoto kabla,jinsi upendo aliokuwa nao moyoni aliushangaa na ilikuwa wazi hakuweza kukaa ofisini bila kupiga simu kumuulizia Abraham ni wazi kwamba alikuwa akitafuta mtoto kwa miaka mingi sana,hata hivyo Marietha pia alimpenda Abraham lakini sio kama Deo alivyompenda.Marietha alivyoandaa kila kitu mezani akamuita mumewe ili kuungana katika chakula cha usiku,ambapo walisali wakimshukuru Mungu kwa kila kitu.Walianza kula taratibu,kwa Marietha chakula hakikushuka vizuri kuna kitu kilimsumbua kichwani kwake,mimba aliyokuwa amebeba tumboni hakuelewa baba wa mtoto ni nani hasa,hilo ndilo lilimchanganya zaidi.
“Marietha,kula chakula”
Deo akamuongelesha,akasogea karibu na kumlisha kwa kutumia kijiko akimuonesha ishara ya upendo mwingi sana aliokuwa nao moyoni,ni wazi kwamba Deo alimpenda pia mkewe na alijihisi ni mwanaume mwenye bahati,mbali na mambo yaliyopita nyuma hakuelewa ingekuwaje kama asingekuwa na Marietha.
“Una tatizo lolote Love?”
Deo akahoji huku akimuangalia Marietha usoni,ni wazi kuwa kuna kitu alikiona ndiyo maana akauliza.
“Hakuna kitu baby”
“Marietha,niambie ukweli.Nini kinakusumbua?”
“Darling sio kitu”
“Ninakufahamu,nje ndani”
“Naelewa”
“Basi niambie nini tatizo”
“Umenisamehe?”
“Kwanini unauliza hivyo”
“Nataka tu kujuwa,mambo yaliyopita bado yananisumbua”
“Achana nayo Marietha,nakwambia kuwa nakupenda.Nimekusamehe na nishasahau muda mrefu sana,kuwa na Amani moyoni.Sawa Darling”
“Ahsante mme wangu,nakupenda sana”
Hapo maongezi yaliendelea lakini bado Marietha hakutaka kuzungumza ukweli wa moyoni,aliogopa kufanya hivyo hakuelewa kwamba atakuwa sahihi au la,bado alihitaji ushauri wa juu ya kitu gani akifanye.Siku zilizidi kwenda mbele na alikuwa akijisikia vibaya, alielewa tayari ni mimba imeanza kumpelekesha puta na siku za usoni Deo angejuwa licha ya yote alijikaza kisabuni.
Ratiba ya Deo siku zote ilijulikana kutoka asubuhi sana na kurudi jioni,hapo Marietha alitumia muda huo kumeza dawa alizoandikiwa,bado swala hilo lilikuwa zito kumueleza mume wake.
Siku moja alivyomaliza kumnyonyesha Abraham na kufanya usafi wa nyumba nzima aliamua kutoka nje ili kupunga upepo,lakini kabla ya kuufikia mlango alihisi kizunguzungu kikali sana,alivyojaribu kujishika na meza alikuwa tayari amechelewa hiyo ilimfanya adondoke chali mzimamzima.
*******
“Noo noo nooo,zile Quotation niletee ofisini kwangu mwenyewe.Hapana Mashala usilete uzushi mimi sifanyi biashara hizo,nilishakwambia nishapiga hesabu na VAT ni Exclusive,sasa tatizo nini?Nimekwambia siwezi kama kuna kitu kin….”
Alikuwa ni Deo akifoka kwenye simu ndani ya ofisi yake huku akipiga piga meza,kitu kilichomkatisha ilikuwa ni simu nyingine iliyokuwa mezani,alivyoangalia juu ya kioo aliona jina na picha ya mkewe,Marietha!
“Subiri Mashala,nitakupigia baadaye”
Alivyokata simu aliyokuwa anazungumza nayo akapokea ya mkewe sababu alijuwa ni muhimu kutokana na mkewe kuwa na mtoto mdogo nyumbani,hiyo ilimfanya awe karibu sana na simu za mkewe.
“Yes baby”
Alipokea kwa mbwembwe na kusema maneno hayo.
“Bosi,shikamoo mimi Biko,Mama anaumwa.Tupo njiani tunampeleka hospitali”
Upande wa pili wa simu ulisikika, Biko mlinzi wa getini alikuwa akitoa maelezo kwa bosi wake.
“Anaumwaa?Anaumwa nini?Mpo wapi?Hospitali gani?”
Deo aliuliza maswali mfululizo.
“Hapa Ubungo,hospitali ya Machange”
“Nakuja”
Deo hakutaka kuuliza maswali mengine zaidi,alichokifanya ni kuvuta koti lake na kuliviringisha mwilini.Akachomoka kama mkuki mpaka nje,ambapo huko aliparamia gari lake na kuondoka kwa kasi,lilikuwa ni jambo lililofanya kichwa chake kipatwe na msongo wa mawazo kwani mkewe kuuguwa ghafla na kufanya apelekwe hospitali ni jambo ambalo halikuwahi kutokea,hakuwa ana majibu sahihi aliamini akifika hospitali atapata majibu ya kitaalam,dakika arobaini na saba baadaye alikuwa nje ya hospitali ya Machange iliyokuwa Ubungo maji,akanyoosha mpaka mapokezi ambapo alisema kilichompeleka.Nesi aliyekuwa dirishani akamuonesha ushirikiano.
“Nyoosha wodi namba nne,mkono wako wa kulia”
“Sawa ahsante sana”
Kwa hatua mbilimbili Deo akaanza kutembea na kufuatisha korido ya hospitali mpaka alipovuka mlango wa kwanza,alivyofika wodi aliloelekezwa akasimama na kuangalia juu ili kuhakikisha kama ndiyo hapo,akasukuma mlango na kuzama ndani.Pembezoni kabisa,mwisho wa pembe alimuona Mlinzi wa getini,Biko. Akatembea kwa haraka mpaka alipomfikia ambapo juu ya kitanda alikuwa amelala Marietha na dripu ya maji mkononi.
“Ilikuwaje?”
Deo akauliza bila salamu,alitaka kujuwa nini kilimpata mkewe mpaka akawa sehemu kama hiyo.
“Nilikuwa getini,nikasikia kishindo ndani.Kukimbia naingia ndani nikamkuta Mama kazimia chini,nikaomba msaada kwa majirani ndiyo Mama Muhina akatusaidia kumleta hapa hospitali”
Hayo yalikuwa maelezo ya Mlinzi huku akimuangalia Bosi wake kwa umakini,Deo alimsikiliza lakini bado swala la Marietha kudondoka halikumuingia akilini,lazima kulikuwa kuna chanzo cha kudondoka kwake na kuzirai.
“Mariethaaa”
Deo akaita kwa sauti ya chini huku akizigusa nywele za Marietha taratibu.
“Abeee”
“Vipi,nini zaidi?”
“Sio ki…..”
Kabla ya Marietha kujibu,akatokeza mwanamme mrefu mwembamba amevalia koti nyeupe,shingoni kaning’iniza kifaa cha kupimia mapigo ya moyo,huyu alikuwa ni daktari aliyempokea Marietha na kumfanyia matitabu.
“Habari za saizi daktari?”
Deo alianza kutoa salamu.
“Nzuri tu,za kazi?”
“Salama,mimi naitwa Deo.Huyu ni mke wangu.Kuna tatizo gani?”
Bila kupoteza wakati,usaili ukaanzia hapohapo.
“Tushamfanyia vipimo tayari,utaongozana na mimi ofisini”
“Sasa hivi?”
“Hapana,ngoja nimuandikie tena dawa nyingine”
Kazi ya daktari ilivyoisha wakaongozana mpaka ofisini ambapo hapo Deo alikaribishwa kwenye kiti na kuketi ili mazungumzo yaanze dakika hiyohiyo.
“Mkeo ana mimba ya miezi mitatu na ana homa kali sana”
Moyo wa Deo ukapiga paa!Majibu ya daktari yalimfanya agande kama barafu,bado alikuwa anatafakari kama ni kweli ama amesikia vibaya na sio kwamba mshtuko wake ulihashiria jambo la hatari,Deo alifurahi na wakati huohuo alisikitika sababu Mkewe alimficha kwa kipindi hicho chote.
“Dokta unasema ukweli?!”
Deo akauliza,tena kwa mshangao wa waziwazi.
“Sina sababu ya kukudanganya.Cha kufanya ni kumsihii atumie hizi dawa nitakazokupa,ataruhusiwa akimaliza dripu”
“Ahsante sana dokta”
Siku hiyo Deo alikenua meno yake yote nje,akasimama harakaharaka na kutoka ofisini kwa daktari akanyoosha na kuingia mpaka wodi alilolazwa mkewe,huko alim-miminia hongera zisizokuwa na idadi kamili na kumpiga mabusu ya mashavu.
“Marietha mbona hukuniambia mapema?Ulikuwa unataka kunificha eeh.Ahsante Mungu wangu kwa kila kitu,Mungu huwa anajibu maombi kwa kweli”
Deo alisema kwa furaha mno,hakuelewa kitu gani kinaendelea kichwani kwa Marietha ambaye alionekana kuwa ana mawazo mengi sana.Nusu saa baadaye dripu ikaisha,Marietha akaruhusiwa kwenda kupumzika nyumbani,kuanzia siku hiyo Deo aliwahi kurudi nyumbani na wakati mwingine inaweza kupita siku mbili asiende kazini,hiyo yote ilikuwa ni sababu ya mkewe,alitaka kuwa naye karibu muda wote,kila siku alimshukuru sana Mungu wake na hiyo ilimfanya afanye kazi kwa bidii zote.Akafungua mradi mwingine huo alifungua kwa makusudi yake tena kimnyakimnya,ilikuwa ni saluni kubwa ya kike tena yenye mashine za kisasa,alipanga baada ya Marietha kujifungua amkabidhi kama zawadi yake.Mpaka inakamilika baada ya wiki tano,ilimlia kama shilingi milioni kumi na mbili za kitanzania,mbali na hayo kwake pesa hizo hazikuwa kitu chochote kile,ilimradi Marietha afurahi licha ya yote alijuwa itakuwa kama ni kitega uchumi kingine kwahiyo pesa yake itarudi.Kila mwanamke aliyeona saluni hiyo alitamani kuingia na ilivyofunguliwa watu maarufu nchini kama Vile Wema Sepetu,Lissa Jansen Irene Uwoya,Jaqlin Wolper na wengine wengi walikuwa wakipishana Sinza madukani kwenye saluni hiyo,kila mtu aliisifia sio masihara,Deo alijuwa kuipamba vizuri na ikawa kivutio kwa kila mtu anayepita nje.
Wakati hayo yote yanaendelea Marietha hakuwa anajuwa lolote,ilikuwa ni lazima afanyiwe ‘surprise’ndiyo maana Deo akaweka jambo hilo kama siri kubwa ingawa jambo hilo lilimkereketa lakini alijiepusha na hakutaka kuvunja ahadi yake aliyojiwekea kwamba mpaka Marietha ajifungue mtoto.Siku zilikuwa zinaenda kwa kasi kama upepo,hiyo ilikuwa furaha kubwa sana kwa Deo lakini kwa Marietha alizidi kukonda,mawazo juu ya mimba yalimfanya akose raha ya maisha.Tujaely Mnzava ndiye alikuwa bega kwa bega akimwambia kuwa ni lazima mimba itakuwa ya Deo tu,alimpa moyo.
“Kweli Tuja?”
Marietha aliuliza,akiwa kama mtu aliyekosa imani kabisa.Tumbo lake lilikuwa kubwa tayari na ilibaki miezi miwili tu ili ajifungue.
“Marietha,huyu mtoto ni wa Deo.Wewe si una Sali sana?”
“Ndio”
“Basi muombe sana Mungu wako,Muombe nayeye atakusaidia”
“Sasa ikitokea akiwa wa Amadour?”
“Haiwezekani! Tena kataa hiyo hali kabisa”
Siku hiyo Tujaely Mnzava aliegesha gari yake nyumbani kwa Deo kwa niya ya kupita na kumsabahi shosti yake, Marietha.
“Wewe Abrahaaam,utadondoka hapo.Mtoto mtundu huyuu”
Marietha aliruka na kumuwahi Abraham aliyekuwa anajaribu kujishika na meza,alikuwa tayari anaanza kutembea.
“Tulia hapo,umemsalimia anti Tuja?”
Alivyokuwa anaongea naye,utadhani kweli alikuwa anaelewa vile lakini badala yake Abraham alikuwa akicheka na hapo ndipo uzuri wa mtoto huyu ulionekana waziwazi.
“Anavyocheka kama Deo vile”
Tujaely akatia neno.
“Deo ndio anacheka hivyo?”
“Wewe huoni au?”
“Sijawahi kumuona”
Marietha akaweka mashauzi kidogo lakini alivimba bichwa kusikia mumewe anazungumziwa.Walivyoongea mambo mengi ya hapa na pale Tujaely Mnzava akaaga na kuondoka zake.
Kesheshe lilikuja alipoingia Avin jioni ya siku hiyo,ndiyo akavuruga kila kitu na kumfanya Marietha aanze kuwaza upya.
“Wewe Marietha mbona una hatari namna hiyo?Sasa….mimi nashindwa sijui nikwambie nini”
“Lakini nilikuwa naogopa”
“Sasa utaona siku hiyo mtoto akitoka,Deo akijuwa atakuuwa”
“Tuachane na hayo.Yona mzima?”
“Mzima,anakusalimia.Hapa nimemwambia napitia kwako mara moja”
“Mwambie ahsante lakini asinitupe kiasi hicho”
“Sawa zimefika”
*********
Mwezi mmoja na wiki mbili ndizo zilizobaki ili Marietha ajifungue mtoto.Kwa maana hiyo Deo na marafiki zake walimfanyia Mtoto shopping yaani ‘babyshower’kwa lugha ya kigeni.Kwa kuwa walishajuwa ni jinsia gani,Deo alinunua nguo nyingi za kike,alizunguka katika kila maduka akanunua nguo pamoja na mabeseni,muda wote mwanaume huyu alionekana akiwa mwenye furaha sana,kila wakati alikuwa na Marietha kushoto kwake,alipokuwa Deo basi Marietha pembeni waliongozana kama kumbikumbi,wakati mwingine Deo alienda naye Mpaka ofisini kwake.
“Lazima uwe unafanya mazoezi kidogo Mama Abraham,sasa ukikaa ndani kila siku utalemaa”
“Sasa ndio kila siku?”
“Ndio,inabidi uwe strong.Unatembea hapa na pale unazunguka huku na kule”
“Mmmh,sawa daktari kwa ushauri”
Akaweka utani kidogo!
“Ha! Haa! Haaa! Haaa!”
Wote wakacheka na mazungumzo yao yalifanyika ndani ya ofisi ya Deo,jioni ilivyofika wakaingia ndani ya gari na kurudi zao nyumbani.

**********
Siku zilijisukuma na miezi tisa ilikuwa tayari imewadia zilibaki siku nne ama chini ya kumi ili Marietha ajifungue hivyo ndivyo walivyoambiwa mara ya mwisho na dokta Okama bingwa wa maswala ya uzazi,huyu ndiye alikuwa daktari wa Marietha.Ilikuwa ni siku ya Jumanne tarehe 7 May,saa kumi jioni ndipo Marietha alipopelekwa hospitali ya Lugalo ili asubiri siku zake zimkute akiwa kitandani.
“Utajifungua salama mke wangu.Usisahau kusali.Nakupenda sana,natamani hata kubaki nawewe hapa hospitalini”
Deo alimwambia mkewe siku hiyo alivyomkabidhi hospitalini,alihisi machozi yanaanza kumlenga,hiyo yote sababu alimzoea mkewe kupita kiasi, kiasi kwamba aliona bora abaki hospitalini akae naye lakini ndiyo hivyo tena hakuwa na jinsi.Kujifungua kwa Marietha siku za karibuni ilikuwa kama harusi kwake kwani alianza kuwaalika ndugu jamaa na marafiki zake ili afanye tafrija ndogo ya kumkaribisha mtoto wake wa kike duniani.
“Ndio,ndani ya hii wiki.Kaa mkao wa kula,Ndio ndio.Wakina Ashura Muhija nishamwambia,mwambie na Mtitu pia.Yes yes nataka kumpigia na Melody simu sasa hivi,huyo hawezi kukosa”
Deo alikuwa simuni siku hiyo anatoa taarifa kwa kila mtu wa karibu yake.Alivyomaliza simu ya kwanza akainua tena kupigia watu wengine.
“Dokta Vipi,Bado?”
Usiku huohuo akamuuliza daktari kama mambo tayari.
“Bado,lakini muda wowote kuanzia sasa”
“Ahsante,Ahsante sana”
Usiku wa siku hiyo Deo hakupata hata lepe la usingizi,alimuwaza Marietha na mtoto wake mwingine kiujumla,binamu yake alikuwepo na huyo ndiye alikuwa akimuangalia Abraham baada ya Marietha kwenda hospitalini.Siku zikaenda na asubuhi ya siku iliyofuata,Deo alipokea habari nzuri sana kuwa mkewe yupo leba anajifungua.
“Mungu ni Mkubwa,Ahsante Yesu”
Deo alishangilia na kurukaruka,hapohapo akavaa nguo zake.
“Nakuja kukuchukuwa,upo wapi?Hostel?Mabibo?Sawa nakuja hapo”
Deo alichomoka kama mshale,akazama ndani ya suruali ili akamchukuwe rafiki yake mwingine huko Mabibo Hostel.
*************

Kuhusu maswala ya kupeleka uji,chakula na mahitaji mengine madogo kwa Marietha alilivaa Tujaely Mnzava na alikuwa akimpa moyo na kumwambia kuwa mtoto ni wa Deo,mpaka asubuhi ya siku iliyofuata Marietha anashikwa na uchungu yeye ndiye aliyepiga kelele mpaka madaktari wakatokea na kumuingiza Leba,Marietha alikuwa akijipiga piga mapajani,majasho yanamtoka uchungu wa kuzaa ulimbana hiyo ilikuwa ni dalili tosha ya kuwa mfuko umepasuka na mtoto anatakiwa kutoka tumboni,manesi na madaktari waligongana vikumbo.
“Sukuma kwa nguvu dada,bana pumzi”
Nesi mmoja alisema huku akiwa kwa chini amekinga mikono yake akisubiri mtoto atoke.
“Dada sukuma,usiache.Mtoto anakaribia kutoka”
Marietha akazidi kujikaza akiwa ameitanua miguu yake huku na kule,alibana pumzi na kujikakamua.Alihisi kitu kizito kinatoka ndani ya tumbo lake,akazidi kusukuma zaidi na zaidi.
“Sukuma sukuma,kichwa kimetoka usiache.Sukuma.SUKUMA TENA”
Kichwa cha mtoto kilianza kutangulia huku Marietha akiambiwa ajitahidi kusukuma,mtoto alivyotoka hapohapo akapoteza fahamu zake.
“Ng’aaaa ng’aaaaa ng’aaaaa”
Ni sauti ya mtoto ndiyo iliyokuwa imeenea chumba kizima baada ya kuzaliwa kwa njia ya kawaida.
“Mmmh”
Nesi mmoja akaguna ilielekea kuna kitu kama alikiona.
“Vipi?”Mwenzake akauliza.
“Huyu mtoto,huyu dada mume wake ni nani?”
“Acha maswali yako,mpeleke huyu Mama Wodi namba tatu.Atundikiwe dripu ya Glucose,tafadhali fanya haraka sana”
Hicho ndicho kitu kilichotokea kwa wakati huo.Wa kwanza kupata habari kuwa Marietha kajifungua ni Tujaely Mnzava sababu aliitwa ofisini kwa ajili ya mazungumzo.
“Huyu Marietha ni nani kwako?”
Dokta alianza mahojiano.
“Ni kama dada angu”
“Mume wake yuko wapi?”
“Nadhani atakuja nilimpigia simu,kwani vipi?”
Kuna kitu kisichokuwa cha kawaida Tuja alianza kuhisi.
“Hapana nauliza tu”
“Naweza kumuona mtoto?”
Tujaely akatoa pendekezo.
“Yes,unaweza njoo”
Dokta akasimama na Tujaely akafuata nyuma,wakaingia mpaka kwenye wodi ambalo mtoto aliwekwa pembeni kwenye kitanda kidogo,kwa kuwa chumba hiko kilikuwa V.I.P ilifanya Marietha awe peke yake,kitendo cha kufika kandokando ya kitanda cha mtoto moyo wa Tujaely uliongezeka mapigo,mtoto alikuwa ana nywele za kizungu,mweupe kupita kiasi.
“Eh Mungu naomba iwe ndoto”
Alitamani iwe hivyo lakini ukweli ni kwamba mtoto hakuwa wa Deo hilo lilionekana wazi kabisa bila chenga ndiyo maana hata madaktari pia walikuwa wapo njiapanda,Marietha alikuwa amepoteza fahamu bado hakuelewa kinachoendelea.
“Huyu ndiye mtoto wake?”
Tujaely akauliza kwa hamaki, kabla ya daktari kujibu mlango ukafunguliwa kila mtu aligeuka ili kujua ni nani kaingia.
“Tujaely!”Sauti ikasikika.
Alikuwa ni Deo Karekezi kaingia akiwa mwenye furaha na tabasamu pana mno.



Moyo wake ulikuwa ukipiga sambasoti kwa furaha aliyokuwa nayo siku hiyo alivyoingia ndani ya chumba alicholazwa Marietha baada ya kujifungua,kushoto alikuwa amelala Marietha na kulia kulikuwa na kitanda kidogo chenye kioo ilikuwa wazi kabisa alikuwa amelala mtoto aliyezaliwa,mita chache mbele yake alisimama Tujaely Mnzava,akamsabahi na kutembea kuelekea kitanda cha mtoto kilipo sababu alitaka kumuona kutokana na kumsubiri miezi tisa mizima.Tujaely Mnzava alihisi kutetemeka mwili na aliogopa kwa wakati mmoja mpaka wakati mwingine akavaa viatu vya Deo ili tu asikilizie maumivu,aliamini ni kiasi gani Deo angeumia.
“Mariethaaa”
Deo aliita akiwa amekifikia kitanda cha mtoto aliyezaliwa na mke wake,akaingiza mikono na kumtoa.Alimuangalia mara mbilimbili na kumgeukia Tujaely.
“Mtoto huyu ana nywele laini sana”
Deo akatia neno kwa makusudi lakini moyoni mwake ilionekana kuna kitu anataka kukitoa,Tujaely kwa aibu akaangalia chini sababu hata angeulizwa asingekuwa ana jibu la kushiba.
“Huyu mtoto amekuwaje?”
Deo akazidi kuuliza safari hii alimgeukia dokta.
“Ni mtoto mdogo bado”
Dokta akajibu.
“Hapana,itakuwa labda mmechanganya mtoto wakati wa kujifungua”
“Ndio mtoto aliyejifungua hongera sana”
Swala hilo halikumuingia Deo akilini hata kidogo,haikuwezekana hata kidogo mtoto aliyembeba akawa wake,sawa yeye ni mweupe lakini mtoto alizidi, hata nywele zilikuwa tofauti kabisa,taa nyekundu ikaanza kuwaka kichwani kwake,akamkata Tujaely jicho kali.
“Tuja”
“Abee shemeji”
“Wewe mtoto umemuona?”
“Ndio shemeji.Lakini inabidi tuongee kidogo”
Ni bora hata Tujaely asingesema maneno hayo sababu ilifanya Deo apate alama ya kiulizo kichwani,hapohapo akamuweka mtoto kitandani na kutoka nje ambapo alifuatwa nyuma na Tujaely.
“Deo Deo Deooo”
“Unataka kuniambia nini?”
Deo akageuka na kujibu kwa swali tena sio hivyo, aliuliza kwa ukali na swala hilo lilionekana wazi sababu hata wauguzi na madaktari waliokuwa wanapita kando yao wengine waligeuza shingo.
“Naomba nikwambie kitu”
“Nakusikiliza”
Tujaely aliishiwa pozi, hakujuwa ni wapi aanzie uso wa Deo ulimtisha kwa kiasi cha kutosha.
“De..”
“Mtoto ni wa nani?”
“Nisikilize sasa”
“Mtoto wa nani?”
Lilikuwa ni swali linalohitaji jibu kwa wakati huohuo,Deo aliuliza kwa ukali hio ilimfanya Tujaely ashindwe kutoa jibu,alichofanya Deo ni kuchomoka na kurudi wodi alilokuwa amelazwa Marietha ambapo alimkuta bado hajafumbua macho,akamsogeza daktari pembeni na kuanza kumtingisha.
“Mariethaa,Mariethaaaa”
Marietha alikuwa akivutwa vutwa ili ashtuke.
“Mgonjwa bado hajapata fahamu ala..”
“Kuna kitu nataka kumuuliza”
“Baadaye”
Majibu ya Daktari yalimfanya Deo ageuke na kuondoka zake ambapo nje alikutana na marafiki zake aliokuja nao,hakuwaongelesha aliwapangua na kutoka nje huko aliingia ndani ya gari na kutomea nje ya geti.
**************
Marietha alizinduka baada ya lisaa limoja na nusu tangu ajifungue mtoto wake,halikuwa jambo la kawaida sababu katika zoezi la kuzaa kwake hakuchomwa nusu kaputi.Kitendo cha kufumbua macho yake alikumbana na Tujaely Mnzava anamtizama,katika kumbukumbu zake kurudi aligundua kwanini yupo juu ya kitanda,akahitaji kumuona mtoto wake kwani alitaka kuthibitisha kama wa Deo ama sio.
“Namuomba mtoto”
Akasema akiwa amechoka na alitia huruma,wasiwasi wake ulionekana usoni.
“Pumzika kwanza Marietha”
“No namuomba mtoto wangu”
“Marietha tafadhali”
Tujaely alijaribu kutumia busara zake na hekima zote ili kumtuliza Marietha lakini haikuwezekana kwani juhudi zake zote ziligonga mwamba,hakuwa na jinsi alichofanya ni kumchukuwa mtoto wa Marietha na kumkabidhi,Marietha aliangua kilio kwa sauti ni wazi kwamba mtoto aliyemzaa alikuwa wa Amadour jambo ambalo aliomba liwe ndoto.
“Huy..uu si..o mtoto wa..ngu.Nitamuuwa”
Marietha aliongea maneno hayo kwa uchungu na kutaka kukitupa kichanga lakini Tuajely alimuwahi kwa kukidaka,Marietha alilia machozi akiwa ana uchungu ajabu,hakuelewa ni kitu gani akifanye.
**************

Siku zote katika dunia hii Mapenzi na Pesa ndivyo vinafanya watu wajenge chuki,wauwane na hata kufanyiana unyama, katika watu ambao walijenga chuki na ikaota mizizi ndani yake ni mzee huyu aliyeitwa Chandra,alikuwa ni mfanyabiashara mkubwa kupita kiasi na pesa zake siku zote alizitumia bila mpangilio hiyo ni kutokana na dhuluma.Mzee Chandra siku zote alipiga pesa kwa njia ya dili chafu na pesa hizo hazikuonekana hata kidogo sababu alitumia kula na wanawake pamoja na pombe kifupi alipenda anasa za dunia,kutumia shilingi laki saba kwa siku kwa mzee huyu ilikuwa kawaida sana.Kila alipoenda katika kumbi za starehe alikuwa ana wanawake wazuri pembeni yake,watoto wa kike waliweza kuzitumbua pesa za mzee huyu kisawasawa.
Mzee Chandra alipenda kudhulumu lakini yeye hakupenda kudhulumiwa hata kidogo na aliipenda pesa kuliko mfuko,mpaka anafikisha umri wa miaka 59 alishauwa watu nane waliomtapeli pesa zake.Mwaka 1998 alijuana na Mzee Kapoor na hapo walianza kufanya biashara ya kuuza figo za binadamu wenzao kwa pesa ndefu sana,kwa siku Mzee Chandra alikuwa anapiga pesa ndefu kuliko mwanzo.Akaona hiyo ndiyo biashara nzuri ya kufanya.
“Kapoor ule mzigo vipi?”
Siku hiyo Mzee Chandra alimuibukia Kapoor ofisini kwake akitaka mshiko wake.
“Nitakupa”
“Sawa,siku zinaenda hata wiki iliyopita uliniambia hivyohivyo”
“Usijali Chandra mambo sio mazuri lakini wiki ijayo”
Mzee Chandra aliondoka zake na wiki ilivyokatika akamfuata ofisini tena ili kukumbusha deni lake lakini alipigwa kalenda tena,taa nyekundu ikawaka kichwani kwake akajuwa tayari anadhulumiwa.
“Ebwana niambie unanipa au hunipi?”
Chandra alifoka siku hiyo akiwa simuni sababu alichoshwa na saundi za Kapoor.
“Nitakupa”
“Lini?”
“Nikipata,alafu Chandra naomba ujue kitu kimoja sipendi unikumbushe kitu hiko hiko kila siku.Usiwe kama mtoto”
“Kwahiyo unajifanya mjanja?”
“Nakwambia ukweli”
“Sawa tutaoneshana,utanijua mimi ni nani”
“Usinipige mikwara basi”
“Siku njema”
Tangu siku hiyo Mzee Chandra akakata mguu,hakumsumbua tena Kapoor ikapita miaka mingi sana,Kapoor alidhani wenda yeye ndio bingwa,akazidi kuendelea kufanya biashara zake kumbe haikuwa hivyo kwani kwa muda wa miaka yote hiyo Chandra alikuwa akifikiria ni njia gani atumie amuuwe.
“Mpo wapi?”
“Mburahati”
“Sawa,mkipata saiti nzuri.Muuweni msifanye makosa”
“Sawa”
Ndani ya gari aina ya ‘Pick up’ kulikuwa na vijana wapatao sita walioshiba mikononi walikuwa wameshika mitutu,hawa walitumwa na Chandra ili kumsaka Kapoor ili wamuuwe hapohapo,walikuwa nyuma ya gari ya Mzee Kapoor usiku huo wanamfuatilia bila yeye kujua,mpaka wanafika Kigogo bonde la Mikumi Mzee Kapoor hakujuwa kama anafuatiliwa,akamshusha Issa kwa niya ya kwenda kumpiga risasi afe kisha amtupe kwenye mtaro wa maji unaoenda kwa kasi,watu waliotumwa na Mzee Chandra na wao wakashuka wakiwa na silaha zao mikononi kila kilichokuwa kinaendelea walikishuhudia,wakamuona Mzee Kapoor anatoa bastola hapohapo mmoja wa mijitu hiyo naye akachomoa bastola kisha kuikoki.
“Paaaaaaaa paaaaaaaaa”Akaachia risasi.
************
Risasi mbili zilisikika kwa sauti kubwa, Issa akiwa kwenye mti amefumba macho anasubiria apigwe risasi na Mzee Kapoor ili afe lakini cha ajabu mpaka zinapita sekunde tano nzima hakuhisi aina yoyote ile ya maumivu ingawa mapigo yake ya moyo yalienda mbio,alivyofumbua macho yake alimuona Mzee Kapoor yupo chini damu zinamtoka.Bila kuuliza chochote aliruka kama swala na kukimbia mbio mpaka miguu yake ikawa inagusa kisogo chake na hakugeuka nyuma,alizidi kusonga mbele akiruka vidimbwi vya maji na kukatiza katikati ya mboga za mchicha na matembele akazidi kusonga mbele zaidi bila kusimama akiamini huo ndio ungekuwa usalama wake,mbele yake kulikuwa na giza nene lakini yeye hakujuwa wala hakuelewa ni wapi anaelekea, mpaka alivyofika makaburi ya kintiku hapo akapunguza mwendo kidogo na kuzidi kuendelea mbele zaidi,akaruka makaburi na kuanza tena kusonga na safari,kila alipokuwa anatafakari maisha yake ndipo alipopata nguvu mpya,mpaka alipofika Landa Bar maeneo ya Kigogo,hapo alisimama na kujificha nyuma ya nguzo ya umeme ili avute kumbukumbu ni wapi alipo.Jinsi alivyokuwa anahema hakutofautishwa na mtu aliyetoka kukimbia kilomita kumi.
“Wewe unafanya nini hapa?”
Ilikuwa ni sauti iliyomshtua Issa aliyekuwa amesimama pembeni ya nguzo,alivyotaka kukimbia akadakwa hapohapo mkono.
“Unataka kukimbia uwende wapi?”
Issa alivyotaka kujitoa ilishindikana,mtu aliyemshika alikuwa ameshiba kuliko kawaida na amejazia misuli.
“Unafanya nini hapa?”
Jamaa akazidi kuhoji maswali,akamvuta Issa mpaka kwenye mwanga ni dhahiri kwamba alidhani mtu aliyemshika ni mwizi ndiyo maana alimchomoa mpaka barabarani.
“Haaaa!Kumbe ndio wewe”
Mwanaume aliyeshiba alimjua Issa,alishawahi kumuona katika vyombo vya habari na kwenye mabango, hapohapo akatoa simu yake na kutafuta namba alizokuwa amezihifadhi,kumkamata Issa kwake ilikuwa ni sawa na zali la mentali.Akapiga simu lakini haikupokelewa.
“Tulia hapo”
Issa alikuwa amelazwa chini,ameekewa kifuti juu ya shingo yake hawezi kujinasua tena,akaendelea kupiga simu tena na tena.Kwa kuwa tangazo la Issa lilikuwa na namba mbili hiyo ilifanya mtu huyo atafute namba nyingine.Ilivyoita tu hapohapo ikapokelewa.
“Hallooo”
Sauti ya mwanamke ilisikika upande wa pili.
“Nimempata mtu mliyekuwa mnamtafuta,Issa”
“Umepata Issa?Wewe iko nani?Iko wapi?”
Alikuwa ni Mama Katrina simuni na alishtuka kupita kiasi na moyo wake ukapiga mkambo kwani kumpata Issa kwake ilikuwa ni tiba ya binti yake kipenzi,KATRINA!



Issa alikuwa akitetemeka kwa hofu sana,jasho lilimtoka sababu alijuwa anaenda tena kukutana na kifo alichokuwa amekikimbia,kwa namna ilivyokuwa alishaelewa hatoweza kukipiga chenga!Alilia akimuomba mtu aliyemshikilia amuonee huruma lakini haikusaidia chochote kile,alivyojaribu kujitoa ilishindikana kifuti cha shingo alichogandamiziwa nacho ilifanya aishiwe nguvu zote mwilini, akabaki tu anasali sala zake zote.
***** *********
Dokta Khaila alishtuka kwa kiasi cha kutosha kiasi kwamba akawa anazunguka zunguka huku na kule akiwa ana simu sikioni akimtafuta mumewe ili ampashe habari juu ya kupatikana kwa Issa ili binti yao apone lakini matokeo yake simu haikupokelewa,akajaribu tena na tena.Akili yake haikuweza kufanya kazi sawasawa sababu Katrina alikuwa yupo maututi kitandani na alikuwa amebakisha masaa ama siku ili aage dunia,hakuwa ana matumaini tena.Kupokea simu na kuambiwa kuwa Issa kapatikana ndiyo ilimfanya apate kiwewe.
“Kapoor pokea simuuu”
Dokta alisema mwenyewe huku akipiga piga miguu chini lakini simu haikupokelewa,hakuelewa kuwa mumewe kapigwa risasi sababu alikuwa nyuma ya kila kitu,ulikuwa ni usiku sana ndiyo maana aliogopa kuondoka mwenyewe hapohapo akapata wazo lingine, akaingia mpaka ofisi ya Daktari mwenzake aliyeitwa Rehema Kiswabi huyu alikuwa ni bingwa wa mifupa lakini ni muafrika,jinsi alivyoingia ofisini kwake na kumvuta ilitisha.
“Twende Rehema”
Dokta Rehema Kiswabi bila kujua hili wala lile nayeye akasimama kama mwanakondoo,kuna kitu kilikuwa kinacheza ndani ya akili yake,wenda Katrina tayari amefariki dunia japokuwa alihisi hayo lakini hakutaka kulipa wazo hilo kipaumbele sana,wakaongozana mpaka nje ya geti ambapo waliingia ndani ya gari.Jinsi Dokta Khaila alivyorudisha gari kinyumenyume iliogopesha,ilikuwa ni kasi isiyokuwa ya kawaida,alivyorudisha gia gari ikazunguka kwa mwendo wa ajabu na kutoka mpaka nje ambapo huko aliingia kwenye barabara ya lami.Spidi aliyotoka nayo ilimfanya Dokta Rehema Kiswabi atake kujua chanzo chake.
“Tunaenda wapi Dokta?”
Dokta Rehema akajikakamua na kuuliza lakini hakujibiwa kitu badala yake Dokta Khaila alitoa simu na kutafuta namba za kijana aliyempigia muda mchache uliopita.
“Muko wapi?”
Mkono mmoja juu ya usukani mmoja akiwa ameshika simu sikioni.
“Kigogo Landa bar”
“Ndio ipi?”
“Kigogo ukifika hapa u…”
“Subiri”
Dokta Khaila akakatisha mazungumzo yake,hakuwa mwenyeji wa maeneo ya Kigogo. Hiyo ilimfanya alazimike kumpa simu Dokta Kiswabi ili atoe maelekezo,ikawa ahueni sababu sehemu aliifahamu fika.Gari ikazidi kutembea kwa kasi ya risasi na hata alivyofika kwenye kona Dokta Khaila alilala nayo bila kupunguza mwendo na dakika hamsini baadaye wakawa wamefika Kigogo,hapo Dokta Kiswabi akaanza kufanya kazi ya kutoa maelekezo.
“Kata kushoto”
Dokta akazungusha usukani mzimamzima bila kupunguza mwendo, alimanusura gari iingie kwenye mtaro,akazidi kusonga mbele mpaka walipoona sehemu kuna nguzo nyingi za umeme hapo ndipo alipoambiwa asimamishe gari,akaweka mguu kati!Kwa haraka akateremka na kuanza kuongoza mbele huku akibonyeza bonyeza simu,kabla hajaiweka sikioni akatokea mwanaume mmoja mrefu wa miraba minne,akasimama mbele yao.
“Habari”
“Nzuri”
“Ndio nyie tulikuwa tunaongea kwenye simu?”
“Ndio”
“Twendeni huku”
Dokta Khaila na Rehema wakaanza kumfuata nyuma ambapo aliwapelekwa mpaka chini ya nguzo.
“Je,ndio huyu?”
Issa alikuwa chini amefungwa mikono yake kwenye nguzo.Amri ikatoka mara moja kutoka kwa Dokta Khaila kuwa afunguliwe muda huohuo.
“Pesa yangu?”
Kijana akauliza alivyoona mambo yanapelekwa kwa kasi.
“Twende kwenye gari,haraka”
Wote wakaingia ndani ya gari na safari ya kwenda hospitali ya Aghakhan ikaanza dakika hiyohiyo.Kitendo cha kufika hakukuwa na muda wa mazungumzo hata kidogo,ilibidi Dokta Khaila aanze kwa kumtoa hofu,moja kwa moja wakaongozana mpaka wodi alilolazwa Katrina hajitambui,kweli mtoto huyu mdogo alidhamiria kufa.Issa alivyomuona alishindwa kuamini macho yake,Katrina alikuwa amepungua uzito kuliko kawaida na mashavu yamemuingia ndani.
“Katriinaaaa,Katrinaaa”
Dokta Khaila akamuita binti yake kwa unyonge.
“Katrina,Issa huyu hapa.Fungua macho”
Akasema tena akijaribu kumzindua kutoka usingizini.Mwili wake ulidhoofika mno,uzito wake uliporomoka hiyo ilimuogopesha Mama yake kupita kiasi lakini hata hivyo matumaini yake yalirudi baada ya Issa kupatikana.Katrina alianza kujigeuza taratibu, ilielekea alisikia jina la Issa limetajwa,macho yake yakawa yanafunguka mbele yake akamuona mwanamme amesimama,bado kumbukumbu zake zilikuwa mbali akaanza kuzikusanya kwa pamoja.
“Iss….a”
Katrina akaita kwa sauti ya chini sana kwa udhaifu hiyo ilimfanya Dokta Khaila alie kwa furaha.Mkono wa Katrina ukasogea karibu akamshika Issa.
“Iss…a niw..ewe?”
Akauliza huku akionekana kumuangalia kwa umakini kama mtu asiyeamini.Haikuwezakana hata kidogo kuamini kama kuna watu wenye mapenzi ya kweli kama Katrina,jambo hilo lilizoeleka kuigizwa kwenye filamu za kihindi na hakuna mtu yoyote aliyeamini kuwa kuna watu wa namna hiyo lakini Katrina alidhihirisha hilo waziwazi.
“Ni mimi Katrina”
“Nili..taka ku..fa kwa aji..li yako.Usiondoke baki hap..a Sogea kari..bu mpe.nzi wang..u”
Huo ulikuwa ni ukweli,hakukuwa na uchawi wala ndumba, Katrina alimpenda Issa kuliko maelezo yaliyojitosheleza ndiyo maana akawa yupo tayari kujitoa uhai wake mbali na kumuona Issa mbele yake lakini bado hakuamini ndiyo maana akaendelea kumshika mkono.
“Usio..ndoke”
“Siwezi”
“Lak..ini nina..umwa sa..na”
“Utapona Katrina”
Maongezi waliyokuwa wanazungumza Dokta Khaila aliyasikia na alibaki kimnya akibubujikwa na machozi,aliuzunika kupita kiasi bado hakuamini kama Katrina anaongea na kutabasamu jambo hilo kwake alilifananisha na muujiza.
Kuanzia siku hiyo karibia robo tatu ya Madaktari walimvamia Katrina na kuanza kumfanyia Matibabu ya hali ya juu sana,akawa anaangaliwa kama yai na katika kutibiwa kwake hakutaka Issa aende popote pale,hilo halikuwa na kipingamizi wakawa wanakesha wote wodini.Ingawa bado alikuwa dhaifu lakini alijihisi amepona baada ya kumuona Issa yupo hai,siku zilikwenda mbele na afya yake iliridhisha japokuwa baba yake Mzee Kapoor hakuonekana hospitalini yeye hakujali,kichwa chake kilijaa Issa tupu wala sio kitu kingine!Dokta Khaila alikuwa bize sana akimshughulikia binti yake lakini kilichomtatiza ni Mumewe kupotea katika mazingira ya kutatanisha.Siku mbili nzima hakuonekana na alivyojaribu kupiga simu haikuita kabisa,hiyo ilimfanya aanze kuingiwa na wasiwasi mwingi sana.
Siku ya nne ikawa hivyohivyo,katika siku ya tano hapo ndipo taa nyekundu ikawaka kichwani,ilikuwa ni lazima kuna jambo baya lilimkuta mumewe,ilibidi aanze kumuulizia kwa ndugu,jamaa na marafiki.Hakuna siku iliyomuumiza moyo kama kupokea simu na kuambiwa kuwa mwili wa mumewe uliokotwa bondea la Msimbazi,ukiwa umepigwa risasi,kilichofanya askari watambuwe mwili wa dokta Kapoor ni vitambulisho,vinginevyo hakuna mtu yoyote yule angeweza kuutambua mwili wake.Dokta Kapoor aliokotwa mto msimbazi uso wake ukiwa umevimba na wenye majeraha ya risasi na alikuwa tayari ameanza kuoza.Kilichofanyika ni kupelekwa moja kwa moja Monchwari huko ndipo mkewe alipoenda na kudondoka akilia machozi.Msiba wa Mzee Kapoor uliwaliza watu wengi sana hakuna hata mtu mmoja aliyejuwa nyuma ya kifo cha mzee huyu isipokuwa Issa peke yake,Kila mtu alijuwa kwamba mzee Kapoor alivamiwa na majambazi na kupigwa risasi.
Wakati mazishi yanafanyika Katrina alikuwa bado hospitalini,hali yake haikuwa nzuri sana ndiyo maana alishindwa kuudhuria msiba wa Baba yake mzazi ingawa aliumia sana mtima!Mzee Kapoor aliacha mali nyingi kupita kiasi na akaunti za benki yake zilisoma pesa za kutosha,vitu vyote vilikuwa chini ya Mkewe Dokta Khaila,huo ndio ukawa mwisho wa Mzee Kapoor duniani.
**************
Hali ya Katrina ilianza kuwa nzuri kadri siku zilivyokuwa zinazidi kusonga mbele,mwili wake ulianza kupata nyama na ngozi yake laini ikaanza kunawili, ilikuwa ni tofauti kabisa na alivyopelekwa hospitalini hapo awali,jambo hilo lilikuwa furaha sana kwa Dokta Khaila sababu nyuma ya matibabu hayo mkono wake pia ulikuwepo lakini licha ya yote aliamini fika kuwa bila Issa wenda wangekuwa wanazungumza habari nyingine,hivyo alitoa shukrani nyingi sana.
“Issa shukrani sana”
Siku hiyo Dokta Khaila alisema akiwa wodini,Katrina alikuwa amekaa kitandani anatabasamu na uzuri wake ulionekana waziwazi.
“Ahsante Mama”
“Na ninahaidi nitapenda wewe kama mwanangu”
“Ahsante Mama”
Ndani ya wodi walikuwa watu watatu peke yao na mazungumzo yalifanyika katika hali ya utulivu na furaha sana.
“Issa”
Katrina akaita.
“Naam”
“Nakupenda sana,nataka unioe”
Lilikuwa ni jambo lililomuacha Dokta Khaila kinywa wazi,moyo wa Issa ukapiga mikito ya nguvu kifuani ingawa hakuelewa ni kwanini.
“Issa,tafadhali.Oa binti yangu,anakupenda sana”
Dokta Khaila nayeye akapigilia misumari alivyoona Issa anasuasua.
Katrina aliruhusiwa baada ya hali yake kuwa nzuri kiafya na kuandikiwa dawa ambazo zingempa nguvu,kwa maana alitakiwa kurudi nyumbani lakini hakutaka kurudi mwenyewe,ilikuwa ni lazima awe na Issa popote pale.
“Issa,utakaa nyumbani.Sawa?Mimi taka wewe ukae karibu na binti yangu”
Dokta Khaila alisema maneno hayo wakiwa ndani ya gari na safari ya kwenda Oysterbay kuanza mara moja,kwa kuwa wafanyakazi waliambiwa kila kitu hiyo ilifanya wapike chakula kizuri na kingi,Issa alikaribishwa siku hiyo kama Mfalme na kupewa heshima yake.
Mugisha mlinzi wa getini aliyekuwa anamchongea alivyomuona alitamani ardhi ipasuke aingie ndani ili akimbie aibu,Issa na Katrina wakaingia ndani,wakala msosi wa nguvu!
“Ushaandalia Issa kitanda?”
Dokta Khaila alimuuliza mmoja wa wafanyakazi waliokuwa wanapita mbele yake.
“Ndio Mama”
“Chumba kipi?”
“Kile cha Juu,katikati”
“Mimi ambia wewe andalia yeye kile chumba kubwa”
“Sawa Mama”
“Fanya haraka”
Kilichoendelea hapo vilikuwa ni vicheko na kugonga ‘cheers’ na usiku ulipoingia Issa akataka kupumzika.
“Katrina,Onyesha Issa chumba ya kulala”
Dokta alizunguka mbuyu kidogo lakini hakutaka kusema wazi kuwa Katrina alitakiwa kulala chumba kimoja na Issa hivyo ilitakiwa Katrina ajiongeze.Katrina mbele Issa nyuma wakaanza kupanda ngazi,wote wakaingia chumbani.
Kilikuwa ni chumba kikubwa sana na kilichokamilika,chenye kila kitu ndani.Katrina akamgeukia Issa wake, bado hakuamni kama wapo pamoja chumbani,bila kuuliza chochote Katrina akajisogeza midomoni mwa Issa wakaanza kulana denda taratibu sana,Katrina alikuwa ana midomo ya rangi nyekundu tena milaini kama sufi,ulimi wake ulikuwa ndani kinywani mwa Issa anauzungusha kila pembe,damu yake ikaanza kumwenda mbio kuliko kawaida,akamvuta Issa taratibu mpaka bafuni ambapo huko kulikuwa na ‘sink’lenye maji,akaanza kumvua Issa nguo moja baada ya nyingine mpaka alivyobaki bila nguo,mwili wa Issa ulikuwa ukichemka hiyo ilifanya hisia zake zisafiri umbali mrefu na kufanya ndizi yake isimame kidedea,Katrina akavua nguo zake harakaharaka nayeye kubaki kama alivyotoka tumboni kwa mama yake,wote wakaingia ndani ya sink kwa ajili ya kuoga.Waliendelea kupigana madenda kwa fujo wakiwa ndani ya maji yenye uvugu vugu,moyo wake kidogo uache mwili,mkono wa Issa ulikuwa umepita na kutomasa maziwa yake huku mwingine ukiwa chini ya mgodi,hapo ndipo Katrina alikuwa hoi hajiwezi tena!


*******
ENDELEA KUSOMA HADITHI NA SIMULIZI ZA MTUNZI….EMMANUEL F.KWAY(THE STORY MASTER)

0 comments:

Post a Comment

BLOG