Search This Blog

Sunday, May 31, 2020

BEDROOM PROFESSIONALS SEHEMU YA 3/10



BEDROOM PROFESSIONALS
MTUNZI….EMMANUEL F.KWAY(THE STORY MASTER)
AGE…(18+)
WatsApp…+255718 862176
SEHEMU YA 3 KATI YA 10 MWISHO
*******


Saa saba ya mchana Leila alikuwa ndani ya kijumba kidogo kwa mganga wa Kienyeji,anajielezea
kama yupo kituo cha polisi.Mzee huyu kazi yake ilikuwa ni kumsikiliza kwa umakini huku akiwa anachanganya dawa kwenye vibuyu vyake.Akachukuwa kikombe cha rangi nyekundu akachota maji kisha kuyachanganya ndani ya dawa nyingine iliyokuwa ya rangi nyeusi,akachukuwa majani na kuanza kuyaponda ponda.
“Usijali Mjukuu wangu,unasema kwamba unahitaji mimba yake itoke?”
“Ndio babu”
“Sawa,cha kufanya inahitajika nguo yake ya ndani”
“Nguo yake ya ndani?”
“Ndio,chupi yake.Ilete hapa keshokutwa jioni kabla ya jua la saa kumi na mbili kuzama”
“Baada ya hapo?”
“Niletee kwanza chupi yake”
Leila alitafakari kwa muda kidogo,hapohapo akisimama na kuaga.

****
“Nakwambiaje Deo,hapa duniani zunguka kooote nenda hata ulaya.Hakuna mwanaume asiye cheat, asikudanganye mtu yoyote yule.Ku cheat ni nature yetu wanaume.Believe me or not.Sawa mimi ninampenda Mke wangu lakini nina cheat vilevile.Sijui tupoje sisi wanaume.Ndiyo tulivyoumbwa”
“wewe Masawe acha masihara,basi.Mimi mbona sijawahi kucheat”
“Thubutuuuuuuu,mimi ninakataa hapa,nitakunya hapa na Kibaigwa kwa mafungu mafungu.Wewe hujawai kucheat Deo?”
“Ilitokea tu bahati mbaya siku hiyo nililewa”
“Sasa unataka kuongea nini.Mimi nakwa….”
“Samahani,nikuongeze kinywaji?”
Muhudumu wa Baa ndiyo aliyemkatisha Bwana Masawe aliyekuwa ana bwabwaja akiwa na rafiki yake Deo jioni ya saa moja wana kunywa pombe.
“Niongeze na pia Mletee na huyu ndugu yangu bia nyingine”
“Sawa”
Muhudumu akaondoka kisha baadaye akafika na bia nyingine mbili akafungua na kuweka juu ya meza kisha kuendelea na kazi zake nyingine.
“Ndiyo nilikuwa nakwambia,siku hizi hata wachungaji wenyewe wana cheat vilevile”
“Na wanawake je?”
“Wanawake ni vigumu sana,mwanamke anaweza akakaa miaka hata miwili asimuone mwanaume.Lakini kwa mwanaume kaa wiki mbili au tatu,wewe usifanye mchezo”
Deo na Bwana Masawe waliendelea kunywa pombe siku hiyo usiku ingawa akili ya Deo ilimuwaza mkewe nyumbani.Kila alipotamani kurudi nyumbani kwake stori zilizidi kunoga.
“Embuu embuuuu Deoo,Twende Dagaa dagaa pale Lego”
“Sawa tumalizie kwanza vinywaji hivii”
“Okay”
Ilikuwa imegonga saa tatu ya usiku na iliwakuta baa ya DDC kariakoo,uzuri kila mtu alikuwa ana gari yake hivyo waliwasha na safari ya kwenda Sinza kuanza mara moja,dakika ishirini na tano baadaye walikuwa Sinza,Lego.Wakaweka magari kando na kuchagua sehemu moja iliyotulia ambapo hapakuwa na bugudha hata kidogo.
“Psiiii psiiiiiii”
Bwana Masawe akamuita muhudumu.
“Niletee Kilimanjaro baridi na Serengeti,alafu muite mtu wa Jikoni”
Vinywaji vilivyoletwa mtu wa jikoni akafika kwenye meza yao.
“Kuna kitimoto jikoni?”
“Ndio”
“Leta kilo mbili na ndizi sita”
“Rosti?”
“Ndiyo,itachukuwa dakika ngapi?”
“Arobaini na tano hivi”
“Aya”
Maongezi ya Deo na Masawe yakaendelea huku wakizidi kupooza makoo yao kwa bia.
“Hapa kuna mchepuko wangu mmoja hapa ndiyo napenda kukutana nao.Mtoto mmoja wa kinyasa”
“Hivi Masawe una watoto wangaapi sasa hivi?”
“Deo acha utani leo hujui?nina wawili.Mmoja yupo form six mwingine darasa la saba”
“Duu,hongeraaa sanaaaa.Mimi ndiyo nakaribia kuitwa Babaa”
“Ulishawahi kuniambiaaa,Hongeera sana.Umejipanga vipi?Na usinione hivi Deo nakunywa bia hapa, Nawaza kesho hii pesa niliyotumia nairudisha vipi”
“Tutazungumza siku nyingine,Wife anapiga.Keshaanza kupata wasiwasi tayari.Nimwambie nini?”
Deo alianza kuhaha kidogo,alivyoona simu kutoka kwa mkewe anapiga.
“Usidanganye mwambie ukweli,Leo ni Ijumaa upo kidogo unakunywa utawahi kurudi”
“Atanielewa sasa?”
“Hata kama hatokuelewa ilimradi umemwambia ukweli”
Deo akapokea simu na kuiweka sikioni kwa ujasiri wa hali ya juu.Alikumbana na maswali ya mkewe akitaka kujuwa ni wapi alipo.
“Nitakula ndioo,samahani nipo kwenye kelele.Nipo Legoo,ndani ya nusu saa nitakuwa hapo”
Simu ikakatwa,siku hiyo waliongea vitu vingi sana.Na Masawe alipoanza kulewa kazi yake ilikuwa ni kuwatongoza wahudumu,Kitimoto kilivyoletwa walikula na kushushia na bia.
“Masawe wacha mimiiii niendee,nikifika nitakupigiaaa”
“Deoo Come on,baki hapa bwana sasa unaniacha mwenyewe ndugu yako”
“Hapana wacha niwahi kesho nayo siku”
Deo hakutaka kubaki akainuka kwa kupepesuka na kutembea mpaka lilipokuwa gari lake,akawasha na kurudisha kinyumenyume,akaingia barabarani na safari ya kurudi nyumbani kwake kuanza hapohapo.
Siku hiyo hakunywa kiasi kingi cha pombe,ndiyo maana hata alipofika nyumbani kwake aliongea na mkewe kwa adabu zote,akala kidogo ingawa alikuwa ameshiba akaingia chumbani na kujitupa kitandani.Usingizi ukamchukuwa hapohapo.

****
“Laki mbili hii,nahitaji tu nguo yake ya ndani”
“Una maanisha chupi?”
“Ndiyo hiyohiyo”
“Sawa”
Kijana wa kihuni aliyeitwa Rama alikuwa umbali wa kama mita ishirini kutoka nyumba ya Deo ilipo mbali na hapo alikuwa ni jirani tu,hivyo nyumba ya Deo aliijuwa vizuri.
Kitendo cha kupewa laki mbili ili kuchukuwa nguo ya ndani ya Marietha ilikuwa ni sawa na kuweka kibakuli cha supu mdomoni,jambo hilo lilikuwa rahisi sana kwake,laki mbili zilikuwa nyingi kwa kazi kama hiyo ya kitoto.
“Kila siku anaanika chupi zake uwani,unataka chupi zake ngapi?”
“Moja tu”
“Poa wewe sista nisubiri hapa”
Leila alikuwa kwenye mgahawa wa chakula anatoa maagizo hayo,akamkabidhi Rama shilingi laki moja kama nusu ya malipo ya kazi hiyo kumaanisha salio lililobaki lilikuwa laki moja.
Rama akachomoka na kuanza kutembea huku akimuacha Leila anamsindikiza kwa macho.Nyumba ya Deo ilikuwa inalindwa na mlinzi wa getini hivyo ingekuwa vigumu kwa Rama kuingia bila kuhojiwa maswali,alichofanya ni kupitia geto kwake akachukuwa begi dogo na kuanza kutembea,akalipita geti nyumbani kwa Deo na kuzunguka uwani,akaangalia huku na kule.Kisha kudandia ukuta,akajivuta juu na kuruka ndani.Kitendo cha kutua tu,mbele yake akakumbana na chupi za rangi tofautitofauti zimetundikwa juu ya kamba.Akavuta moja na kuiweka ndani begi.
“Wewe Rama,unafanya nini hapa?”
Lilikuwa ni swali la Deo baada ya kutokeza mlango wa uwani,jambo hilo lilimfanya Rama aanze kutetemeka kijasho kilianza kumtoka.
“Mama,Mamaa aliniita.Marietha aliniambia nije kuchukuwa uchafu”
“Kuchukuwa uchafu?Mariethaaaaaa”
Deo hakuwa na uhakika, majibu aliyotoa kijana huyu ambaye hata siku moja hakuwahi kumuona ana mazoea na mke wake yalimtia mashaka licha ya yote hakuwahi kumuona ndani ya nyumba yake.Ndiyo maana akamuita Marieta ili atoe majibu.
“Wee Mariethaaa”
“Abeeee”
“Njoooo”
Ndani ya sekunde tano Marietha alikuwa mlango wa uwani ametanda,anamwangalia mwanaume aliyekuwa nje amesimama kama m-masai aliyepoteza shuka lake.
“wewe ndiyo umemuita Rama aje kuchukuwa sijui uchafu?”
“Mh,Mimi?Hapana mimi sijawahi kuongea naye”
“Wewe nani kakutuma?”Deo akauliza kwa ukali.
Rama alihisi nguo yake ya ndani inaanza kulowana hakujuwa kama mkojo ama jasho!



Macho yote yalikuwa kwake,Marietha na Deo walikuwa wakimtizama wanasubiri jibu aliloulizwa kwamba ametumwa na nani ndani ya nyumba hiyo sababu mara ya kwanza alimtaja Marietha ndiye aliyemwagiza akatoe uchafu akidhani kwamba Deo angemezea na kumwambia kuwa aende lakini ilikuwa tofauti kabisa na alivyodhani kwani Deo alimuita Mkewe na kumuuliza swali hilo na badala yake Marietha alimkana hapohapo.
Rama hakuelewa ni kitu gani akifanye, ukweli ni kwamba alitumwa achukuwe nguo ya ndani ya Marietha ili amaliziwe salio lake la laki moja kama malipo ya kazi hiyo ndogo kwake,kusema ukweli kulimaanisha kukosa pesa hiyo ambayo kwake ilikuwa ni kama ya bure.Alimtizama Deo na mkewe ambao wote walikuwa wametanda mlangoni,sura ya Deo ilimtisha.
“Nani amekutuma wewe Rama?Si naongea nawewe”
Deo akauliza tena.Deo alijichanganya kitu kimoja kumuita mlinzi wa getini.
“Nani kamfungulia huyu geti?”
Mlinzi akachapwa swali lililomfanya ababaike sababu katika kumbukumbu zake hakukumbuka kama alimfungulia mtu yoyote yule geti asubuhi hiyo.
“Hapana bosi,mimi sijafung….”
Hapohapo Rama akachomoka kama mkuki akampiga mlinzi kikumbo kikali,akatoka mbio akiwa ameshika vizuri begi lake, akaparamia geti na kutoka zake nje.Hakuna hata mmoja wapo aliyeelewa Rama amefuata nini.Kwa Deo alidhani kwamba kijana huyo alitaka kuiba, akampuuzia na kuingia ndani hakuwa na sababu ya kumfuatilia kiundani.

*****

Kama alivyohaidiwa na ndivyo ilivyokuwa,Rama alikabidhiwa kiasi cha shilingi laki moja kisha Leila akachukuwa nguo ya ndani ya Marietha yaani chupi,akaiweka ndani ya mfuko wa nailoni akatafuta taxi na kurejea hotelini ili asubiri muda usonge apeleke mzigo aliotumwa kwa mganga wa kienyeji,muda wote alitabasamu na kuelewa kwamba tayari yeye ni mshindi na Deo angekuwa wake lazima.Tangu azaliwe katika maisha yake hakuwahi kudhani kwamba mapenzi yana nguvu namna hiyo,akabaini kwamba watu wanaweza hata kuuwa kwa ajili ya mapenzi.Saa kumi jioni juu ya alama ilivyotimia alitoka nje na kukodi taxi ambayo ilimpeleka mpaka Chanika kwa mganga wa kienyeji.
***
“Nifuate Mjukuu wangu”
Mganga wa Kienyeji ambaye alikuwa ni mzee mwenye mvi nyingi kichwani alitoa kauli hiyo akimwambia Leila.Wote wakasimama,ilikuwa tayari imetimu saa moja jioni,giza lilikuwa lishaanza kutanda.
“Usiogope mjukuu wangu nisubiri hapo”
“Sawa babu”
Babu akazunguka nyuma ya kibanda chake kisha kutokeza na babu mwingine mzee kama yeye,wakatembea mpaka kwa Leila kisha kuanza kuingia katikati ya miti mingi.Mkononi babu alishika kigoda na chungu.Na mwenzake alikuwa ameshika mishumaa ya rangi nyekundu mitatu,mkaa pamoja na dawa nyingine kwenye vibuyu.Walivyofika njia panda safari yao ikaishia hapo,dawa zikawekwa chini mishumaa ikawashwa.Yakachukuliwa mawe matatu moto ukawashwa kisha chungu kikawekwa juu ya mafiga.Babu akamimina dawa na maji kiasi ndani ya chungu kisha akatoa dawa nyingine inayofanana na unga,akaweka ndani ya maji ambayo yalianza kuchemka.Wakati hayo yanaendelea yeye Leila alikuwa anatetemeka anaogopa sana,wazee hawa wawili waliendelea kufanya kazi yao.Baada ya hapo unga mwingine mweusi ukamiminwa ndani ya chungu kisha Babu akaanza kuponda ponda majani,akayatumbukiza pia ndani ya chungu.
Baada ya dakika kumi na tano maji yalikuwa tayari yamechemka.Babu akachukuwa kikombe kilichozungushiwa kitambaa cheusi,akachota maji kidogo.
“Kunywa hii”
Leila alikabidhiwa kikombe.Kilimuunguza kwa mbali lakini alijikaza,akaweka kikombe mdomoni akaanza kunywa kama mtu anayekunywa chai.
“Maliza yote”
Babu akasema tena, Leila akaendelea mpaka maji yalipoisha ndani ya kikombe.
“Mjukuu wangu kama nilivyokwambia mara ya kwanza wewe ni mchafu,inabidi usafishwe vua nguo zako”
Kauli hiyo ilimshtua Leila akabaki anashangaa kana kwamba hakusikia alichoambiwa,kuvua nguo zake zote ulikuwa mtihani mwingine tena mbele ya wazee wawili.
“Mjukuu wangu,vua nguo zako”
Kwa uwoga akafungua zipu ya dera mgongoni,likateremka chini.Kutokana na kuwa na mimba kubwa kiasi ndani hakuwa na kitu chochote,alijisikia aibu kupita kiasi lakini hakuwa na namna yoyote ile.
Wazee hawa waliipua sufuria kutoka kwenye mafiga na kuliweka chini ambapo ulichukuliwa wembe ukaanza kupakwa dawa,Leila akaanza kuchanjwa mgongoni na wembe.Yalikuwa ni maumivu mengi lakini alivumilia sababu alikuwa ana shida,moyoni alianza kujuta kufanya kitu kama hicho sababu hakuelewa kwamba mambo yangekuwa kama hayo.Alivyomalizwa kuchanjwa,akaanza kumwagiwa maji mwili mzima, akasafishwa na majani yaliyokuwa ndani ya sufuria.Wazee hawa walifanya hivyo huku wakizungumza kwa lugha zao za kiganga.Chupi ya Marietha ikatolewa na kutumbukizwa ndani ya sufuria,baada ya dakika moja ikatolewa, wakaanza kumsugua nayo Leila mgongoni.Zoezi lilikamilika ilivyofika saa mbili na dakika thelathini usiku,Leila akafunikwa na shuka jekundu mwili mzima,akashikwa mkono na safari ya kurudi kilingeni kuanza.

Hakuona mbele kutokana na shuka kumziba mpaka usoni hata hivyo giza tayari lilikuwa jingi,walitembea kwa hatua kama ishirini ndipo walipofika kwenye kibanda cha mganga.
“Tayari tusha kusafisha kilichobaki ni kukupika”
Leila alibaki kimnya mwili wake ulikuwa ukimsisimka sio masihara,mapigo yake ya moyo yalikuwa yakidunda kama kitenesi.
“Lala hapo juu ya mkeka chali,fumba macho ukiona kitu chochote useme”
“Sawa babu”
Leila akafumba macho yake na alichokuwa anakisikia kwa wakati huo ni maneno kutoka kwa wazee hao ambao walikuwa wanaongea kwa lugha zao za kiganga.
Leila aliendelea kufumba macho yake huku akitetemeka ajabu,hakuelewa ni kitu gani ambacho ataenda kukiona.Dakika kama kumi zilivyopita akaanza kuhisi kama upepo unampuliza kichwani na miguuni hapo ndipo hofu ikazidi kumtanda zaidi.Hakuamini alichokiona mbele yake,alimuona Deo akiwa uchi wa mnyama yupo mbele yake,akashindwa kuelewa kwamba ilikuwa ni ndoto ama ni kweli Deo alivutwa kichawi.Hapohapo akakurupuka na kufumbua macho yake.
“Tayari nimeona kitu”Akasema,wazee wakasitisha mazungumzo yao.
“Umeona nini?”
“Nimemuona Deo”
Wazee wakatizamana na kutabasamu,kilichomshtua zaidi Leila ni wazee hao ambao hawakuwa na meno yaani vibogoyo kabisa.Leila akasogezwa na kupewa kitu kama fimbo ambayo juu yake ilikuwa na irizi.
“Sema chochote unachotaka”Babu akamwambia Leila.
Akasogea karibu na kijiti na kutamka maneno ya kimapenzi kuhusu Deo na mwisho akahitimisha kwamba Mimba ya Marietha iharibike na awe tasa maisha yake yote,asizae.
****

“Hata kama. Wewe si unajuwa mimi nimeoa,nina mke wangu nina muheshimu”
“Deo hata kama,mimi pia nina mume isitoshe nina mtoto vilevile lakini nimekumisi Deo wangu”
“Hapana Olivia”
“Please Deo,alafu sikutegemea kukuona tena nikajua bado upo Uingereza.Deo still nakupenda”
“Olivia,sikia naendesha gari naenda ofisini sasa hivi,naomba tuongee badaaye”
“Unafanya kazi wapi? Deo naomba nije nikuone tafadhali”
“Posta,Samora Avenue ulizia Transcontinental General Supplies.Karibu na jengo la Nissan”
“Nissan?lile jengo la vioo?”
“Yes,ukifika hapo nipigie simu.See you”
Deo alikata simu haraka sababu mbele yake aliona askari wa usalama barabarani, kuonekana anaongea na simu huku anaendesha gari ingemlazimu alipe faini ama akalale kituo cha polisi kwa maana hiyo hakutaka swala hilo litokee, kuna makosa mengi ya kufanya ambayo hayaepukiki lakini hilo ilibidi ajiepushe nalo,akaweka simu chini akanyoosha mguu akaipita maktaba kuu ya taifa,mbele kidogo akakunja kulia na kuzidi kuendelea na safari.
Baada ya dakika kumi na tano akawa anaweka gari nje ya jengo kubwa la Mkapa karibu na benki ya CRDB.
Hapo ndipo alikuwa anaegesha gari lake kisha kuzunguka jengo la nyuma yake.Akavuta koti lake na kuanza kutembea mpaka ndani,alisalimiwa na wafanyakazi wake akanyoosha mpaka ofisini kwake.
“Niletee kahawa”
Deo aliagiza kupitia mkonga wa simu na baada ya dakika moja sekretari wake akatokeza akiwa na kikombe kilichokuwa juu ya kisosi.
“Karibu bosi”
“Ahsante”
Sekretari akaishia zake.
Akiwa ameweka kikombe cha kahawa mdomoni ghafla akahisi kama amepulizwa shingoni na upepo,akaweka kikombe chini.
Akageuka nyuma lakini hakuona kitu,alihisi nywele zake zinamsisimka kupita kiasi,akasita kidogo.Kwa macho ya kawaida hakuweza kuona nyuma yake, kwenye kona walikuwa wamesimama wazee wawili wenye mvi wameshika usinga wanampiga nao kichwani na kumpuliza shingoni.
kitendo cha kuweka kikombe cha kahawa juu ya meza babu mmoja akasogea na kumimina ungaunga mweupe.Alifanya hayo akijuwa kivyovyote vile Deo hawezi kumuona na hata kama angeingia mtu yoyote wasingeonekana sababu eneo hilo zima walikuwa wamemwaga dawa zao za kiganga aina ya zizila, kazi yao ilivyoisha wakapotea kwa njia ya kuyeyuka.
Deo akavuta kikombe cha kahawa na kuendelea kuinywa.
“Griii griiii”
Simu yake ilimshtua na aliyekuwa akipiga sio mwingine bali ni Olivia,akaichukuwa na kuipokea, akaiweka sikioni.
“Yes”
“Nipo Nissan hapa,nielekeze Deo”
“Upo na gari au?”
“No,kwenye bajaji”
“Mwambie akulete jengo la Mkapa”
“Poa”
Simu ikakatwa.
Kazi ya Deo ilikuwa ni kujaza makaratasi aliyokuta mezani,akavuta kompyuta na kuingiza ‘data’ kwa ajili ya kuifadhi kumbukumbu za kazi zake.
Hazikupita hata dakika tano simu yake ikaita tena,ilitoka kwa Olivia alivyoipokea kazi yake ilikuwa ni kumuelekeza.
“Subiri hapohapo nje nakuja”
Deo akasimama na kukata simu,akatembea na kuvuta mlango akatoka nje ambapo alimuona Olivia.
“Huku Olivia njoo”
Mwanamke mnene kiasi mrefu,alimgeukia Deo, alivyotabasamu meno yake yalikuwa yamejipanga vizuri na katikati alikuwa ana mwanya.Alikuwa ni mwanamke mrembo ambaye alishawahi kuwa mpenzi wa Deo miaka kumi iliyopita,ilikuwa kama Muujiza kukutana tena sababu Olivia alidhani Deo hatorejea tena nchini Tanzania,kilichowafanya waonane tena ni kongamano la Uwaridi lililowakutanisha wafanyabiashara na wajasiliamali mbalimbali pamoja na waandishi wa vitabu maarufu kama Eric Shigongo,Suleiman Kijogoo na akina Ibrahim Gama!
“Pita ndani”
Deo akasema na wote wakaingia ofisini.Deo akapita mpaka kwenye kiti chake.
“Deoo,hivi ni wewe ama naota?”
Olivia bado hakuamini mtu anayemuona mbele yake.
“Ndiyo mimi”
“Umekuwa mkubwa,zamani haukuwa na ndevu”
“Miaka imeenda sana Olivia,vipi familia haijambo?”
“Haijambo mtoto wangu sasa hivi ana mwaka,anaitwa Beatrice”
“Wacha weee”
“Ndiyo hivyo Deo,una ofisi nzuri.Nakumbuka ulikuwa unaniambia ni lazima uje kumiliki ofisi.Finaly ndoto zako zimetimia”
“Si unajuwa Olivia,binadamu siku zote lazima tuishi kwa ndoto”
“Hongera sana,nakumbuka vitu vingi sana nikikuangalia”
“Unakumbuka nini?”
“Kitandani,maneno yako,Mapenzi yako.Still nakupenda Deo”
“Hapana Olivia”
Deo aliweka ngumu lakini Olivia siku zote hakuwa mwanamke mwenye aibu hata siku moja hilo Deo alilijuwa sababu kipindi cha mapenzi yao alikuwa akimpiga madenda mbele za watu hata ingekuwa stendi ya basi Olivia angetoa ulimi wake na kupigana denda.Hicho ndicho kilichotokea, Olivia akasimama kutoka alipokuwa na kuzunguka upande wa Deo.
“Olivia unataka kufanya nini?hapa ni ofisini ja…”
Kabla ya Deo kumaliza anachotaka kusema,shingo yake ikashikwa akageuzwa.
Olivia akamfuata midomoni akatoa ulimi wake,wakaanza kubadilishana mate kwa njia ya ndimi.Mkono wa Olivia ukapita chini na kuanza kupapasa koki ya Deo ambayo taratibu ilianza kutuna,mwanamke huyu hakuishia hapo.
Akasukuma kiti cha Deo kwa nyuma akapiga magoti na kufungua zipu ya Deo.
“Olivia una una taka kufanya nini lakini?”
Deo aliuliza,sio kwamba hakuelewa kitu kinachotaka kutokea lakini hakuwa na uwezo wa kuzuia jambo hilo sababu alianza kuhisi damu yake inamwenda mbio,mwili wake ulimsisimka.
Hasa Koki yake ilivyotolewa na kuwekwa mdomoni,katika michezo ya kucheza na maiki basi Olivia alikuwa fundi hodari kuliko kawaida,alikusanya mate mengi mdomoni mwake akawa anailamba,akaibugia maiki ya Deo iliyokuwa imesimama kama mnara.Kazi ya Deo ilikuwa ni kushika nywele za Olivia huku akihisi vitu vinatembea mwilini mwake.Alisahau kwamba yupo ofisini kwake na jambo alilokuwa analifanya lingemshushia heshima zake endapo angekutwa na wafanyakazi wake.Olivia aliendelea kuchezea koki sio mchezo,huku akizidi kuichuwa,kadri alivyozidi kufanya jambo hilo ndiyo damu ya Deo ilizidi kumwenda kasi.
****

“Bosi Yupo lakini ana mgeni”
“Ni muhimu sana”
“Subiri kidogo”
“Okay”
Leila alikuwa mapokezi akimuulizia Deo,alikuwa na dawa zake kwenye mkoba alioshika.Ilikuwa ni lazima aipake juu ya meza ya Deo na nyingine ampake mkononi, hivyo ndivyo alivyoambiwa na Mganga wa kienyeji kwa masharti ya kwamba isionekane.
Dakika mbili nzima zilikatika,uvumilivu ukamshinda.
Bila kuruhusiwa akasimama wima akidhani wenda Mwanamke wa mapokezi alipewa maagizo na Deo kwamba akifika yeye asiruhusiwe kuingia.Akanyoosha,akakunja kona na kuufikia mlango wa Deo akasukuma,kitu alichokutana nacho mbele yake kilifanya mapigo yake ya moyo yapige kwa nguvu.Alikuwa ni Deo amekaliwa kwa juu anafanya ngono na mwanamke mwingine, kwa mshtuko wa ajabu akadondosha mkoba ukafunguka.
Vitu vilivyokuwa ndani ya mkoba wake kama kibuyu kidogo na irizi vikatokeza nje.Moyo wake ukapiga paa!Kwa sababu Deo alikuwa akiutizama mkoba, hapo ndipo Olivia nayeye akageuka ili kujuwa ni nani aliyekatisha starehe yake.


Deo alikuwa amefumaniwa ‘live’ tena bila chenga.Leila alisimama bado mlangoni hakuwa anaamini kile anachokiona.Alimuheshimu Deo kuliko mwanaume yoyote yule ambaye alishawahi kumjua katika maisha yake lakini leo hii anamuona mbele yake anafanya mambo ya kihuni naya kishenzi tena bila kukosa adabu ndani ya ofisi yake.
Ingawa hakuwa ana mahusiano naye ya kimapenzi lakini moyo wake ulimuuma ajabu.Wakati huo Olivia na Deo walikuwa wakiweka nguo zao sawasawa,Olivia akapandisha sketi yake Deo akawa anafunga mkanda vizuri.
“Le le le Leila”
Deo akaita akiwa na kigugumizi kilichompata ghafla,hakujuwa kimetokea wapi sababu hakuwahi kuwa nacho.
“Deo,Real?”
Leila akauliza kwa njia ya kushangaa.Moyo wa Olivia ulianza kukita sio masihara,katika akili yake alijuwa kwamba mwanamke aliyesimama mbele ni mke wa Deo ndiyo maana aliogopa kupita kiasi,hakuelewa ni kitu gani akifanye ndiyo maana akabaki kimnya.
“Leilaa,huyu hap..”
“Shut up Deo,Shut up..Nampigia Mkeo namwambia kila kitu.Subiri uone”
“Leila sikiliza nikwambie”
“Nikusikilize nini?”
“Usifike huko tunaweza tukamalizana tu”
“Hapana,umalizane na nani? Malaya wa kiume wewe, Son of a bitch”
Hasira za Leila zilichanganyika na wivu ndani yake,kitendo cha kumuona Deo anafanya ufuska na mwanamke mwingine kilimchanganya akili yake kuliko maelezo yaliyojitosheleza povu likamtoka,akawa anaongea bila breki kwa jazba,akaingiza mkono ndani ya mfuko wake wa dera na kutoa simu ya mkononi.
“Ngoja nimpigie mkeo,nimueleze aje hapa sasa hivi”
Leila alikuwa akipiga mkwara ukweli ni kwamba hakuwa na namba za Marietha na hilo alilijuwa wazi kabisa lakini alifanya hivyo ili kumtisha Deo aliyekuwa mbele yake ana haha kama mtuhumiwa aliyefunguliwa mashtaka ya kumbaka mkwewe.
“Lakini da….”
Olivia alivyotaka kuingilia alitulizwa.
“Tena wewe kahaba,Keep your mouth shut.Coward,unanifahamu mimi?”
Ilikuwa ni kama anamsubiri mwanamke huyo atie neno ili ambwagie matusi yote aliyokuwa nayo kutoka ndani ya kifua chake.Akazidi kumtukana matusi ya nguoni tena kwa sauti ya juu.
“Stupid asshole,Bitch.Malaya mchafu yaani umetoka huko unapotoka umekuja kutom** ofisini huna hata thamani,hujioni”
“Leila….”
“Nawewe nyamaza,kahaba wewe.Unataka kumtetea huyo Malaya wako sio”
Leila akazidi kupayuka mpaka sauti ikatoka nje, wafanyakazi wakasikia.
“Dada sikia ujue nimekuvumilia sana,kuwa mstaarabu basi”
Olivia akasema,alionekana kukasirika kwa mbali.Alivyoongea maneno hayo ilikuwa ndiyo kama kamwaga mafuta ya petroli kwenye moto.
“Nani awe mstaarabu? mimi au wewe?”
“Wewe mshirikina mkubwa.Na tunguli zako”
Olivia aliongea maneno hayo huku akitizama chini,dawa alizopewa ili kumroga Deo zilikuwa juu ya malumalu.
Hilo ndilo lililomfanya Leila aishiwe pozi lakini hakutaka kulionesha swala hilo waziwazi,akazidi kurusha matusi makali kama kisu.Deo aliyekuwa pembeni alivyojaribu kuingilia nayeye alichanganywa vilevile, akaogeshwa matusi.Hapo ndipo kama chui Olivia akachomoka na kumvaa Leila, wote wakadondoka chini.Kilichosikika hapo vilikuwa ni vishindo vya watu kupigana makonde.
“Jamani huko kwa bosi kuna kitu,unasikia vishindo”
Mmoja wa wafanyakazi wa Deo akaacha kubonyeza kompyuta,akatega sikio lake kwa umakini sana.Ni kweli maneno makali yalikuwa yanapenya kwa kila mfanyakazi.
“Kweli.Embu ngoja niende”
Kijana mmoja aliyeitwa Faraji alisimama lakini kabla ya kufika mlangoni kwa bosi wake,mlango ukafunguliwa Deo akatoka nje.
“Niitie askari haraka sana Faraji”
Deo akasema maneno hayo huku majasho yakiwa yanamtoka,mambo yalikuwa mazito tayari.
Leila na Olivia walikuwa chini wanagaragazana wakipigana makofi, alishindwa kuwaamulia ndiyo maana alitoka nje ili kutafuta msaada wa walinzi kutoka nje.Walinzi wawili wakaingia ofisini,Kilichowashtua ni baada ya kumkuta Leila yupo chini anavuja damu puani,usoni amechanwa na kucha ndefu za Olivia.Walinzi wakawaachanisha,wafanyakazi nao hawakucheza mbali wote walitoka kwenye meza zao na kuingia ofisini kwa Deo ili kushuhudia, hawakutaka kupitwa na umbea.
“Malaya wewe,Nye** zako unaleta mpaka ofisini”
Leila alitoa maneno makali sana akiwa ameshikiliwa na Mlinzi mmoja kwa nyuma.
“Nawewe jee,si ukakunwe na mumeo aliyekupa mimba hiyoo,mbwa wewe”
“Mbwa babako na mjomba wako,na kama hujui sasa hii mimba ni ya Deo…Atazunguka kote hapa atarudi tuu”
Wanawake hawa walitupiana maneno makali kupita kiasi,kauli ya mimba iliwafanya wafanyakazi wote wajiulize maswali mara mbilimbili.
Kwa Deo alipuuzia sababu alijuwa Leila yupo katika hasira na mambo aliyokuwa anaongea yalisababishwa na ghadhabu.
“Watoe wote njee,chukua huu mkoba wa Leila.Watoe nje,washenzi hao”
Deo alisema huku sura yake ikiwa na makunyanzi,sio siri alichukia kwa kiasi cha kutosha na tukio lililotokea ndani ya ofisi yake lilikuwa ni aibu kubwa tena ya mwaka!kwa mtu mzima kama yeye na aliyekuwa na heshima zake ndani ya ofisi mpaka jamii nzima inayomzunguka hakupaswa kufanya kitu kama hicho na kwasababu hiyo hakutaka tena kubaki ofisini,aliangalia chini kwa aibu na kurudi ofisini kwake akachukuwa funguo za gari na kutoka nje bila kusema lolote.
Na hata alivyofika nje aliwakuta Olivia na Leila wanatupiana maneno makali.
“Nyie wapumbavu,tokeni ofisini kwangu.Wewe askari watoe ili eneo wakatukane huko mbali kabisa,washenzi wakubwa nyie”
Deo alisema kwa ukali na kutembea mpaka alipoliacha gari lake,akaingia ndani na kuliwasha,akarudisha kinyumenyume na kuondoka zake,hakutaka kujuwa nini kiliendelea huko nyuma!

*****
Bado Mungu alikuwa anayapigania maisha yake,isingekuwa Dokta Philiphs Zagarino kufika nchini Tanzania kwa nia ya kuonana na Dokta Khaila akitokea nchini India, basi maisha ya Issa yangekuwa hatarini zaidi,hapo ndipo dokta Khaila alipoomba msaada mwingine,wakishirikiana na mumewe.Hapakuwa na kipingamizi chochote,Issa akaingizwa tena ndani ya chumba cha upasuaji.Muda wote moyo wa Dokta Khaila ulikuwa ukipiga kwa nguvu,aliogopa mno na kitendo cha mgonjwa kufia katika hospitali yake kingefanya C.V zake kuchafuka.Ndiyo maana alipambana mpaka mwisho kujitahidi.
Siku hiyo usiku wa saa tatu ndipo Issa alirudishwa ndani ya chumba cha upasuaji,wakishirikiana na dokta Philips Zagarino huyu alikuwa ni mzungu kutokea barani Ulaya lakini maisha yake yote alilia nchini India,huko ndipo Dokta Khaila na mumewe walisomea udaktari wakajuana naye.

Taa kubwa ikawashwa Issa akachomwa sindano ya nusu kaputi,kichwa chake kikaanza kufumuliwa upya.Ndani kulikuwa na jopo la madaktari nane wanafanya kazi hiyo kwa umakini wa hali ya juu sana!
“Nipatie huo mkasi na pamba”
Dokta Philips akasema kwa lugha ya kiingereza,hapohapo akakabidhiwa vifaa hivyo.Kichwa cha Issa kilikuwa kimechanwa tayari.Madaktari walikuwa makini mno na kilichowafanya wajuwe kama mgonjwa wao ana uhai ni mashine ya mapigo ya moyo iliyokuwa inapiga kelele.
“Nipe huo mkasi.Hapana, huo hapo mwingine mdogo”
Asilimia themanini ya upasuaji huo ulifanywa na daktari wa kizungu na kilichogundulika ni kwamba ndani ya ubongo wa Issa damu ilivulia na kulikuwa kuna uvimbe,jambo ambalo lilimshtua sana Dokta Philips, haikuwezekana hata kidogo kwa mgonjwa mwenye matatizo kama hayo awe anaishi mpaka siku hiyo.
Na hata alivyomaliza kuutoa uvimbe na kutoa damu iliyovulia aliendelea na utafiti mwingine,kila kitu kilikuwa kimekamilika ndani ya lisaa limoja na nusu,Issa akashonwa na kichwa chake kikarudishiwa kama kilivyokuwa awali.
Baada ya kazi hiyo kufanyika Dokta Philips akatoka nje akavua koti na kutoa kitambaa kilichokuwa kimeziba mdomo na pua yake.
“Kila kitu kipo sawa,nadhani mpaka kesho asubuhi atakuwa amezinduka matumaini yangu kuanzia hapo unajua cha kufanya”
Maelekezo hayo alikuwa anapewa dokta Khaila wakiwa wanatembea kwenye korido.
“Sawa nitalisimamia hilo zoezi Dokta”
“Nashukuru, usiku mwema”
“Dokta Philips”
Kabla hajaufikia mlango Dokta Philips alisimama baada ya kusikia anaitwa,akageuka.
“Ahsante kwa kila kitu”Dokta Khaila akasema huku akitoa tabasamu mwanana.
Dokta Philips nayeye akatabasamu lakini hakujibu chochote na kutoka nje,hiyo ilimaanisha kwamba kila kitu kipo sawa kabisa.

****
“Hapana umekosea masharti,siwezi kukusaidia.Mambo haya tumeongea sana tu.Tena tukakubaliana kuwa dawa hizi asizione mtu yoyote yule”
Mambo yalikuwa yameharibika kwa Leila, alikuwa amekosea masharti na Mganga alikuwa amechukizwa kwa kiasi cha kutosha sababu hata yeye alijuwa kivyovyote vile mambo mabaya yangemrudia.
Kukosea masharti katika uganga kulimaanisha adhabu kubwa kutoka kuzimu,babu huyu alikuwa ni Mganga mkubwa na upande mwingine alikuwa ana nguvu za kichawi na mkuu wake alikuwa ni Lusifa ama Shetani Subiani.Jambo la kukosea Leila masharti kulimfanya akasirike mno na hakutaka kumuona tena.
“Nimekwambia ondoka,na baada ya siku mbili lazima ufe”
Babu huyo alihitimisha na kutoka zake nje,akiwa amekasirika sana.Leila alikuwa peke yake analia machozi,mambo aliyoambiwa yalimtisha na pia vitu vilikuwa vinamtokea puani,alijuta kujiingiza kwenye maswala ya kishirikina na hata siku moja hakudhani kama mambo yangekuwa magumu kiasi hicho,alivuta kamasi na kulia kwa kwikwi.
“Bado upo?”
Babu alivyoingia alifika na usinga,akamkaripia.
“Ba..bu nia..mbie kitu ga..ni niki.fanye”
“Huna kitu kingine cha kufanya ni lazima utakufa tu”
“Ba..bu nisa..mehe”
Leila aliendelea kulia,macho yake yalikuwa mekundu mno na yalimvimba.
“Subiri hapo”
Babu akasimama na kuwasha mshumaa mwekundu,akavuta kitambaa chekundu na kutoka nje ambapo alitembea mpaka katikati ya kichaka, mwendo wa kama hatua thelathini,hapo alikutana na mti mkubwa wa mbuyu,ulikuwa una mizizi mikubwa,akapiga magoti na kuweka mshumaa chini na kuuwasha.
Akaanza kuongea maneno ya kiganga,akasimama na kuanza kuuzunguka mbuyu,alivyofikisha mara tatu.Akasimama na kupiga tena magoti.Upepo ukaanza kuvuma.
“Unataka nini unatakaaa niniiii?”
Ilikuwa ni sauti nzito iliyokuwa inajirudia mara mbili kama mwangwi ikitokea ndani ya mbuyu.Babu akatoa maelezo yake na mwisho akahitimisha kwamba anahitaji kusamehewa kwa jambo alilolifanya.
“Ha ha ha ha ha ha haaaaaaaa!”
Sauti hiyo nzito ikacheka,kisha upepo mkali ukaanza kupuliza mithili ya kimbunga,mshumaa ukazima.Mtu aliyetokea mbele yake alitisha kupita kiasi,kichwani alikuwa ana pembe moja,sikio moja la paka na lingine la mbwa.Kucha za jitu hilo zilikuwa ndefu kupita kiasi,na alivyocheka meno yake yalikuwa yamechongoka na marefu kama misumari ya nchi nane.Ulimi wake ulikuwa mrefu tena mwembamba kama nyoka,ukaanza kumlamba lamba babu huku akimzunguka akiwa kama anamkagua.
“Ha ha ha ha ha ha ha ha haaaaaaaaa,Unajuwa cha kufanya.Inahitajika damu ndiyo usamehewe damu ya kafara,baada ya wiki moja hahahahaha”
Jitu hilo likapotea hapohapo.
Babu akasimama akarudi kilingeni ambapo alimkuta Leila ameinama analia machozi.
“Kamata hii dawa,leo ukilala iweke chini ya mto.Haya mafuta jipake baada ya kuoga.Leo usiku saa sita na dakika moja ole wako usifanye hivyo”
“Sawa ahsante babu”
****
“Ahh sshss aaah De…o aaaah don’t St..op”
Ungekuwa dirishani unasikiliza ungesema wenda Marietha alikuwa akifanya makusudi kutoa sauti hiyo ya puani kumbe alikuwa katika raha zilizozidi kipimo,miguu yake ilikuwa huku na kule imetanuliwa.
Deo yupo juu yake wanafanya tendo la ndoa usiku wa saa tano baada ya kula chakula na ilielekea alikuwa anakaribia kufika mshindo sababu alikuwa anaukwaruza mgongo wa Deo,huku akiwa kama anamng’ang’ania na kumvuta zaidi.
“Ah ah ah ahh Deooo aaaaaaaah”
Hapo ndipo ulikuwa mwisho wa safari ya Marietha kufika mlima kitonga,Deo alikuwa bado na alikuwa akisubiri mkewe afike kwanza.Harakaharaka alianza kukizungusha kiuno chake ili nayeye afike kileleni,mkewe alikuwa ana mimba kubwa hivyo alifanya naye ngono kwa nia ya kupanua njia na kumridhisha vilevile.
“Aaah!aaah”
Deo nayeye akatoa sauti ya ki utu uzima baada ya kupasua yai la bata,akajitoa kwa mkewe ili asilale kifuani mwake kama alivyozoea siku zote, aliogopa kuligandamiza tumbo la Marietha.
Kwa uchovu wa tendo hilo Marietha alisimama na kuingia bafuni ili kujimwagia maji,akafungua mlango na kuwasha ‘switch’ ya taa.Mwanga ukatokea,akafungua bomba la mvua.Kuna kitu alianza kuhisi,mwili wake ulimsisimka na kuhisi kama nywele zake zimemsimama, haikuwa hali ya kawaida hata kidogo,akasitisha zoezi la kupaka sabuni ili kusikilizia, katika hali ya kushangaza akahisi kuna mkono wa mtu umemshika begani!




Jinsi Marietha alivyoshtuka hata Deo ilimuogopesha hiyo ilifanya kidogo ateleze kwenye malumalu.
“Vipi?”
Deo akauliza sababu yeye ndiye aliyetokeza bafuni na kumshika begani.Mapigo ya moyo ya Marietha yalikuwa yakipiga kwa nguvu,bado alikuwa anaogopa! Deo alimtisha akakishika kifua chake ili kuyahisi mapigo yake yanavyoenda mbio.
“Embu sikiliza mapigo yangu ya moyo yanavyoenda”
Marietha akachukuwa mkono wa Deo akauweka kifuani mwake.
“Nini kimekuogopesha?”
“Wewe hapo baby,siku utaniua ujuwe”
“Pole”
Kilichofuata hapo bafuni ni kuogeshana na kucheza michezo ya ki utu-uzima.Kazi ya Deo ilikuwa ni kumsugua mgongo mkewe na alivyomaliza mkewe akamfanyia mumewe hivyohivyo kisha kuanza kupigana madenda,lilikuwa ni bafu kubwa la kisasa wapo ndani ya yakuza.Marietha ameshika kitu kama mkonga wa simu kumbe ni bomba la kisasa linalotoa maji mithili ya mvua inayonyesha,wakafanya hivyo na walivyoridhika wakaingia chumbani kulala!
“Nyauuu nyaauuuu nyauuuuu”
Usiku wa saa saba paka walisikika wakilia nje,hiyo ilikuwa dalili mbaya sana, jinsi paka hao walivyolia iliogopesha sababu wengine walilia kama watoto wadogo.Deo na Marietha walikuwa wamelala fofofo hii ni baada ya wazee hawa wa kichawi kuingia kutokea kwenye kona na kupuliza dawa iliyoitwa pumbazo hii wachawi wengi huitumia ili kufanya mtu alale na dawa hiyo ilikuwa na uwezo wa kumfanya mtu aote ndoto nzuri.
Wazee hawa wawili waliangalia huku na kule na kuendelea kupuliza madawa ndani ya chumba cha Deo.Babu mmoja akatembea mpaka kwa Marietha,akashika kibuyu vizuri na kukiweka kichwani kwa Marietha,akampaka dawa usoni kisha akarudi kinyume nyume mpaka ukutani,akawa kama mtu anayeita mtu kwa njia ya ishara.Kwa nguvu za kichawi Marietha akatoka kitandani lakini huku nyuma aliacha kivuli cha mtu,kwa macho ya kawaida ndivyo ilivyokuwa kumbe ulikuwa ni mgomba,Marietha na Wazee wawili wa kichawi wakapotelea kwenye pembe ya ukuta.

Yalikuwa ni mambo ya kutisha lakini ndiyo ulikuwa ukweli halisi kwamba wazee hawa walitumia usafiri wa fisi kupaa angani.Marietha akiwa katikati Babu mmoja mbele na mwingine nyuma, walikuwa ni kama wapo kwenye pikipiki iliyopakia mshkaki huku babu wa mbele akiwa anatumia usinga, ilionekana huo ndiyo ulikuwa kama usukani.Ulikuwa ni usafiri wa haraka sababu walifika chanika kwenye kibanda chao ndani ya dakika mbili,wakamtua Marietha na kuanza kumchezea ambapo walimpaka dawa tumboni na kumchanja chanja mgongoni,wakamtoa nywele zake kidogo za kichwani.
“Arapata aru aru aru”
Hayo ndiyo maneno yaliyosikika kutoka kwa babu huyu wa kichawi, Marietha akapigwa kofi la shavu,hapohapo akapotea!
***
Wa kwanza kuamka alikuwa ni Deo ili awahi kibaruani,akamuacha Marietha kitandani sababu hakutaka kumsumbua,alinyoosha mpaka bafuni,huko alipiga mswaki na kufanya kila kitu.Alivyotoka alikuwa tayari keshaoga,akapita mpaka kabatini na kuanza kuchagua nguo atakayovaa siku hiyo kazini.Haikuwa kawaida hata kidogo kwa Marietha mpaka wakati huo asiwe hajayafumbua macho yake japo waongeleshane.Hilo lilimfanya Deo amuangalie mkewe aliyekuwa amelala chali fofofo kwa kama sekunde tano nzima huku akiwa anafunga vifungo vya shati lake.
“Naona leo umelala sana”
Deo akasema ili kujaribu kama Marietha alikuwa anamsikia lakini ilikuwa ni kama anajiongelesha mwenyewe,mkewe hakufumbua macho mbali na hapo wala hakujigusa hata kidogo.Alivyomaliza kuvaa viatu ilibidi amsogelee.
“Marietha,Marietha”
Akaita huku akimtingisha.
“Mh!”
Marietha aliguna lakini alikuwa bado ameyafumba macho yake.Ni kweli,alihisi amechoka vibaya sana alishindwa hata kuyafumbua macho yake kabisa.
“Baby sasa hivii saa ngapi?”
Marietha aliuliza kwa sauti iliyojaa uchovu wa hali ya juu lakini alikuwa bado ameyafumba macho yake.
“Saa tatu sasa hivi,vipi hali yako?Mbona leo umelala sana?”
“Nimechoka sana Love”
“Mambo ya jana nini?”
Deo akaweka utani kidogo,akawa ana maana kwamba mechi ya usiku wa jana yake ndiyo iliyomfanya awe hoi bin taaban.
“Hahaha kwenda huko”
Marietha akatabasamu na kujigeuza upande wa pili,mwili wake aliuhisi umechoka kuliko kawaida.Hakujitofautisha na mtu aliyetoka kulima heka saba shambani,sio mwili tu kuchoka bali alihisi homa kwa mbali lakini aliipuzia sababu alijuwa kwamba ni mambo ya mimba.
“Baby lakini najisikia homa homa hivi”
Safari hii Marietha aligeuka na kuyafumbua macho yake.
“Nikupeleke hospitali?”
“Hapama usijali nenda kazini,nikizidiwa nitakupigia simu”
“Sawa Wife,mimi naenda”
Kama siku zote inavyokuwa,Deo akamsogelea mkewe mdomoni na kumpiga busu.
“Kazi njema”
Marietha akasema huku akimuangalia mumewe anavyofungua mlango na kutoka nje,mwili wake aliuhisi hauna nguvu na alianza kuhisi baridi,akavuta blankenti na kujifunika gubigubi.

****

“Halloo Mama shikamoo,ndiyo ndiyo huku salama Mama.Kama nilivyokueleza wiki iliyopita kuhusu hali ya mke wangu,leo ndiyo unaanza safari?Nashukuru sana mama yangu.Ndio, unakuja na Dada Eva?Nitafurahi sana aya safari njema nadhani kesho utakuwa umeingia tuzidi kuwasiliana”
Deo alivyokata simu akaiweka mezani kisha kuendelea na majukumu ya kiofisi, alikuwa simuni anazungumza na mama yake akiwa ndani ya ofisi yake nyuma ya meza kubwa iliyokuwa na kompyuta juu yake,akashusha pumzi ya ndani kwa ndani na kuendelea na shughuli zake za kila siku.
****
Wakati binadamu wenzake kama yeye wamelala usiku yeye alikuwa ndani ya chumba kidogo cha mganga anapikwa kichawi,Leila alinuwia kumteka Deo mazima na kabla ya hapo mimba ya Marietha iharibike na asizae tena yaani amfunge kizazi sababu alijuwa hiyo ndiyo ingekuwa kiunganishi chao endapo mtoto angezaliwa,hakutaka swala hilo litokee hata kidogo labda awe amekufa.
Ndani ya kibanda kulikuwa na chungu kikubwa chenye maji ya baharini na majani ya mti uliopondwa pondwa yaliyoitwa mkaratusi pamoja na majani ya mkuyu, haya yote yalikuwa yamepondwa pondwa na bado mganga alikuwa anamimina dawa zake ndani ya chungu hiko huku msaidizi wake ambaye pia alikuwa ni mzee alikuwa akikoroga maji hayo.
Leila akakatwa baadhi ya nywele zake pamoja na kucha. Vikafungwa ndani ya kitambaa chekundu kisha kikatumbukizwa ndani ya sufuria,likawekwa juu ya mafiga maji yakaanza kuchemka.Ilivyofika dakika kumi na tano maji yakawa tayari.
“Vua nguo zako uwende ukaoge haya maji,pale nje huku ukisema kitu unachotaka”
Hivyo ndivyo Leila alivyofanya,akatoka nje na kuvua nguo zake ambapo alibaki mtupu.Maji yakaletwa akaanza kuoga nayo huku akitamka maneno ya kimapenzi kwa Deo na mwisho akahitimisha kwamba Mimba ya Marietha itoke na amchukie kuliko kinyesi,alivyomaliza kuoga akapewa mafuta awe anajipaka kila usiku.
“Hakikisha huu mkono unampa Deo.Huu wa kushoto nasisitiza tena wa kushoto.Baada kupaka hii dawa usimsalimie mtu yoyote yule,ni Deo peke yake tena asubuhi ya kesho na mapema”
“Sawa”
“Kazi itakuwa imeisha,baada ya hapo ukifanikiwa ndiyo uje tuzungumzie malipo”
“Sawa babu”
“Kila la kheri”
“Ahsante babu”
“Lala hapo,kisha kesho saa kumi na mbili uanze safari ya kuondoka”
Ulikuwa ni usiku mnene kumaanisha kwamba hakukuwa na usafiri wa aina yoyote ile,hivyo Leila alilazimika kulala ndani ya chumba kidogo cha mganga wa kienyeji akisubiri kesho yake kukuche ili aende zake,masaa yalisogea kwa mwendo wa ajuza na kulivyokucha alidamka akamuaga babu wa kiganga kisha akaanza kuingia katikati ya miti mingi,akatokea barabarani.
Hapo akatoa simu yake na kumpigia dereva taxi ili amfuate na kumrudisha hotelini sababu huko alitaka kubadilisha nguo apake dawa mikononi na kumuibukia Deo ofisini kwake,ampe mkono ili kazi yake ianzie hapo.
****
Saa kumi na moja jioni Deo aliweka gari yake kwenye maegesho maalum ya magari,ndani ya stendi ya Ubungo, alikuwa akimsubiri Mama yake mzazi ambaye alikuwa amepanda basi la kampuni ya Falcon,ambalo safari yake ilianzia nchini Uganda kupitia boda ya Mtukura kisha kuingia Bukoba ambapo hapo Mama Deo ndipo alipopanda basi hilo,kutokana na urefu wa safari ililazimika watumie siku mbili nzima sababu walilala njiani.

Siku iliyofuata tangu azungumze na Mama yake simuni ndipo alipoamua kufika Ubungo ili kumsubiria sababu dakika thelathini lililopita nyuma alifanya naye mazungumzo kwamba alikuwa Kimara baruti, hiyo ndiyo ilimfanya awashe gari na kunyoosha mpaka Ubungo ili amuwahi Mama yake mzazi,muda wote usoni alikuwa mwenye tabasamu sababu alimpenda sana Mama yake kuliko kiumbe chochote kile duniani.
Alitoka ndani ya gari na kutembea mpaka sehemu yalipoegeshwa mabasi hayo ya kampuni ya Falcon.
“Kaka mambo vipi?Hapa ndiyo mabasi ya Falcon yanapaki?”
Deo alimuuliza muuza magazeti aliyekuwa pembeni yake ingawa alijuwa ndiyo hapo lakini alitaka kuhakikisha.
“Ndiyo”Akajibiwa.
Hazikupita hata dakika kumi,akasikia mlio wa honi wa basi akageuza shingo yake nyuma ambapo aliona basi kubwa ambalo ubavuni limeandikwa FALCON COACH,akaachia tabasamu pana zaidi na kusogea karibu.Ambapo basi hilo lilifika na kupiga breki,kama kawaida ya ubungo wabeba mizigo walifika mlangoni ili kuwadandia abiria wanaotaka huduma zao.
“Taxii taxiiiii”
Madereva taxi nao hawakucheza mbali waliwaita abiria,ili wajipatie walau riziki zao.Deo alisogea taratibu mpaka mlangoni akiwa na kihoro huku macho akiwa anayatupa dirishani kuangalia kama atamuona Mama yake mzazi,macho kwa macho wakagongana na mwanamke mweupe mnene kiasi, wote wakatabasamu na kupungiana mikono huyu alikuwa ni dada yake mkubwa aliyeitwa Eveline,lakini walizoea kumuita Eva,nyuma yake alikuwa Mama yake mzazi.Wote walitabasamu hata kabla ya kushuka ndani ya gari.Mama Deo na Eva walikuwa na furaha kwa kiasi cha kutosha,kwanza walifika salama alafu pili walifurahi kumuona Deo kwa mara nyingine,wakavuta mabegi yao madogo yaliyokuwa juu sehemu maalum ya kuwekea mizigo midogo na kuanza kushuka chini ambapo walikumbana na madereva taxi.
“Mama taxi,Mama Mizigo weka huku”
Madereva taxi na wabeba mizigo wakaanza kuwagasi.Hapo ndipo Deo aliwapangua na kumsogelea Mama yake akamkumbatia kwa furaha.
“Mama…Shikamoo pole na safari”
Alivyomuachilia Mama yake, akamsogelea dada yake na kumkumbatia kwa furaha vilevile.
“Eva,nimekumisi dada yangu,karibu sana.Hakuna mizigo mingine?”
“Ipo kwenye buti”
“Wapi hapa au kule?”
“Kule kwa nyuma”
Kondakta wa basi hilo akaitwa na kufungua buti la gari ambapo mizigo ilianza kushushwa.
“Na hilo gunia hapo”
Mama Deo akasema.
“Hili?”
Kondakta akauliza akiwa ndani ya buti huku akigusa gunia moja wapo.
“Sio hilo.Hilo la juu”
“Hili?”
“Ndiyo”
Gunia likashushwa na mabegi mengine yakateremshwa.
Akaitwa mtu kubeba mizigo akaiweka juu ya kitololi chenye matairi mawili kwa chini huku wakianza kutembea kuelekea kwenye maegesho ya magari.
Lilikuwa ni kosa kubwa kumpa m-beba mizigo mabegi bila kupatana bei,kichwani kwa kijana huyo alijuwa tayari ni lazima alikuwa amepata bingo na jinsi alivyomuona Deo amevaa suti hapo ilikuwa ni lazima aondoke na wekundu wa msimbazi yaani elfu kumi.
“Wapi broo?”
Kijana akauliza huku akiburuza kitololi chenye matairi.
“Hapo kwenye hiyo gari nyeusi Verosa”
“Sawa kaka”
Walivyofika, kijana akaanza kushusha mizigo.
“Bei gani?”
Deo akauliza huku akianza kujisachi mifukoni.
“Hapo kumi na mbili broo”
“Niniiiii?”
Deo akauliza kwa hamaki akiwa ameukunja uso wake,sio kwamba hakusikia.Bei ilimshtua mno.
“Elfu kumi na mbili”Kijana akarudia.
“Una wazimu nini?na sisi tulipanda humohumo au?”
“Sio hivyo broo,tunalipa ushuru hapa getini”
“Acha kelele shika hii”
Deo alitoa noti ya shilingi elfu mbili na kumkabidhi kijana m-beba mizigo.
“Broo bado”
“Ebwana usinisumbue,nitakuitia mwizi sasa hivi.Unataka elfu kumi na mbili?yanini?na taxi bei gani?”
Deo aliijuwa pesa mbali na hapo kitendo alichotaka kufanyiwa kilimkera sana sababu kichwani kwake alitafsiri kwamba alionekana yeye wakuja ama mshamba wa jiji ndiyo maana akachukia mno,akaingia ndani ya gari huku Mama yake mzazi pamoja na dada yake kuingia pia,wakamuacha kijana anatoa matusi,ilikuwa kidogo Deo amshukie ampige makofi.
“Acha mwanangu,achana naye achana na hao wavuta bangi”
Mama akamtuliza mwana,Deo akapiga gia na kuondoka zake.
“Hilo gunia lina ndizi mwanangu,mimi mwenyewe nitakuwa nawapikia”
“Ahsante Mama pole na safari.Eva vipi mbona husemi kitu?”
Kilichokuwa ndani ya gari ni vicheko na furaha,hata walivyofika nyumbani furaha ilizidi, Marietha alivyowaona aliwachangamkia na kumrukia wifi yake kwa furaha.
“Oh wifi hongera sana”
Eva akatoa pongezi huku akishika tumbo la Marietha,Mama mkwe ndiyo usiseme!Muda wote alikuwa akicheka kwa furaha akamsahau mwanaye Deo.
“Mkwe wangu,hujambo?Za masiku?Jamani hongera sana”
“Ahsante Mama shikamoo,ngoja nikusaidie kushusha mabegi”
“Ah hapana,mwache Deo afanye hiyo kazi.Mimi nawewe twende ndani”Siku hiyo ilikuwa nderemo na vifijo kwenye familia hii,sio Mama wala dada wote walimpenda Marietha kupindukia na walifurahi kumuona.
Nyumba ilikuwa kimnya lakini siku hiyo furaha iliongezeka maradufu!



“Irene yeye ndiyo amegoma kuja kabisa?”
“Yupo shule anakaribia kufanya mitihani,likizo alikuwa tuition”
“Mungu atamsaidia atafaulu”
“Hapendi kusoma mpaka abuluzwe na viboko”
Irene alikuwa mdogo wake Deo wa mwisho.Katika familia yao walizaliwa watoto watano baba mmoja mama mmoja lakini wawili walifariki na wakabaki watatu Deo,Eva na Irene.Watoto hawa walipendana kwa kiasi cha kutosha.Deo ndiye alikuwa wa kwanza katika familia ya Mzee Karekezi yeye ndiye aliyekuwa mtoto wa kiume wa pekee akifuatiwa na mdogo wake wa Kike aliyemuachia ziwa aliyeitwa Eveline.
Mama yao alikuwa Mhaya kutoka Bukoba kijiji cha Ngala,alikuwa ni Mama aliyewalea kama mwanajeshi alikuwa ni mkali kuliko shubiri Mama Deo hakutaka mchezo,alikuwa akicheka na mtu dakika moja lakini haikumchukua sekunde sura yake kubadilika,ndiyo maana Deo alitokea kumuogopa sana Mama yake kuliko baba yake mzee Karekezi.
Ingawa alimtelekeza Mama yao akaenda kwa mwanamke mwingine lakini hakuacha kumpenda!
“Mimi mwenyewe mbona nilikuwa hivyohivyo Mama”
“Eh ila wewe ulikuwa kiboko,ulikuwa mbishi sijui nini kilikubadilisha”
“Nayeye atabadilika tu”
Mama na mwana walikuwa wakiongea seblen kwa furaha.
Kwa wakati huo Marietha alikuwa chumba cha wageni anamuonesha wifi yake chumba cha kulala na kila kitu nyumbani hapo.
“Hiki ni chumba chako,Mama yeye atalala chumba kinachofuata”
Marietha aliongea kwa uchovu,mimba ilikuwa kubwa tayari.Pembeni alikuwa amesimama Eva anaangalia huku na kule anakikagua chumba, kilikuwa chumba kizuri na kikubwa.Mbele yake kulikuwa na kabati kubwa la kuhifadhia nguo hapo ndipo alipotembea na kuweka begi lake ndani ya kabati.
“Alafu nimesahau,huku bafuni.Utatumia hili sink lile kule bovu,nitamwambia Deo kesho alete fundi atengeneze”
“Ahsante sana wifi,kapumzike tu wewe niachie mimi”
Marietha akatoka na kutembea mpaka seblen,kwa heshima zote akamuita Mama yake mkwe ili akamuoneshe sehemu ya kupumzika.
“Hapana pumzika,Deo inuka ukanioneshe chumbani kwangu.Alafu inabidi mtafute housegirl humu ndani,wewe Deo.Kwanini usifanye hivyo?”
Mama kabla ya kusimama akamtizama Deo akiwa katika sura ya umakini kidogo.
“Atakuja,hii wiki”
Deo hakutaka maongezi yawe marefu ndiyo maana akaongea maneno hayo kwa nia ya kuepuka kuhojiwa zaidi sababu swala hilo alikumbuka alishawahi kumwambia Mkewe akakataa katukatu.
“Aje bwana,huoni hali ya mkeo”
“Sawa Mama atakuja”
“Aya nipeleke chumbani kwangu”
Siku hiyo nzima Deo alikuwa akifanya kazi ya kuweka mazingira ya nyumbani sawa,akawaonesha vyumba vya kulala ndugu zake na kila kitu kilivyokamilika, Eva akaingia jikoni ili kuandaa chakula cha usiku,ambapo alipika ndizi Bukoba na senene waliotoka nao kijijini kwao,siku hiyo walichelewa kulala sababu walikuwa na mengi ya kuzungumza.

Mama alisimulia jinsi Bukoba kulivyokuwa,Mara Mama Mutashobwa kaiba Mbuzi wa Babu Kuboko ili mradi muda uwende.Na ilikuwa ikitoka stori hii anaingiza jambo lile,ili mradi wote walikuwa wakicheka,upande mwingine wa Mama Deo alikuwa ni mcheshi na anapenda utani ndiyo maana kila baada ya dakika tano watu waliangua vicheko.
Marietha alipenda sana kucheka akatoa mpaka machozi na mbavu zikawa zina muuma.
“Yule Mzee alikutwa bandani kwa Mzee Kuboko anaiba Mbuzi.Na huyu Kabarira alikuwa anabaka nguruwe sijui alichanganyikiwa,wakamkuta bandani kwa Mzee Chura,alitolewa akaambiwa hayaa mbebe mpenzi wako hivyo hivyo ulivyo"
Hizo ndizo zilikuwa stori za Mama Deo na wanae siku hiyo usiku na walilala saa nane ya usiku.

***

Tangu Mama yake pamoja na dada yake wawepo nyumbani alikuwa mtu wa kurudi mapema sababu aliwaheshimu, alirejea nyumbani kila ifikapo saa tisa alasiri na ilikuwa ni lazima mkononi awe amebeba chochote, kama siyo nyama basi samaki.Wote walimfurahia,hata Marietha alichangamka sababu alipata watu wa kumuongelesha hata hivyo tangu Mama yake mkwe awepo nyumbani hapo hakuwahi kufanya kazi yoyote ile,alikuwa kama malkia,Eva na Mama yake mkwe walimsaidia kazi zote kama kufua,kupika na kuosha vyombo.
Sio siri walimpenda mkwe wao na hata wao vilevile walikuwa na hamu ya kumuona mtoto atakayezaliwa ndiyo maana waliapia kwamba hawatobanduka jijini Dar es salaam mpaka Marietha ajifungue.
“Huyu mtoto wa kiume alafu”
Mama Deo alianza kutoa utabiri siku hiyo baada ya kumchunguza Marietha kwa kitambo kidogo.
“Mh Mama umejuaje?”
“Nimekuangalia tu usoni alivyokuharibu,kakutoa chunusi. Mara ya mwisho nilivyokuona haukuwa hivyo ulikuwa softi.Huyo mtoto atakuwa ana hasira sana alafu”
“Mimi ningependa awe mtoto wa kike”
“Basi mimi nakwambia huyo wa Kiume”
“Basi kheri”
Siku hiyo walikuwa nje uwani wanapunga upepo,hapo ndipo Mama Deo alipopata nafasi ya kumuhadithia Marietha enzi zake za zamani na tangu alivyompata Deo na kumsomesha.
“Baba yake aliniacha kipindi Deo yupo fom five,huyu Eva yupo fom three,niliumia sana lakini kama mwanamke nilisimama imara nikashindana na changamoto”
Mama alifunguka maisha yake yote,mpaka alivyomsomesha Deo kwa shida akiwa anauza senene, akafaulu vizuri na kuchaguliwa kwenda kusoma Uingereza na wadhamini,kwake ilikuwa kama ahsante Mungu.
“Alaf…”
“Hee Mama kumbe mpo huku?”
Deo ndiye aliyeingilia kati akiwa ametanda mlangoni anamtizama Mke wake pamoja na mama yake wakiwa wapo kwenye bustani ya maua wanapunga upepo.
“Shikamoo Mama”
“Marahaba,niko na mwanangu hapa tunapiga stori”
“Mh aya bwana,Eva yeye yuko wapi?”
“Atakuwa chumbani kwake”
“Basi mimi nipo chumbani,naenda kupumzika”
“Aya sisi tupo”

***

“Ah ah ah De..o ah ah ah ah ssshss aaaaah hivy..o”
Leila alikuwa chini, Deo juu yake tena anakizungusha kiuno kama muimba mziki maarufu nchini Tanzania H-Baba,na vitu alivyokuwa anahisi ndani ya mwili wake havikuweza kuelezeka kiwepesi hata kidogo.Deo alikuwa juu yake Nyoka yupo shimoni na wakati huohuo yupo mdomoni mwake wananyonyana midomo,mambo yalikuwa ni raha mustarehe kwa Leila na aliamini kwamba dawa zake tayari zilikuwa zimefanya kazi,mbali na hapo alikuwa ana mimba yake tumboni baada ya hapo aliamini kwamba swala la kuiharibu mimba ya Marietha lilikuwa ndiyo jambo lifuatalo,wakati akiwa chini chali miguu yake imetanuliwa huku na kule alikuwa akitafakari vitu vingi sana,hususani jinsi ya kumteka Deo kimapenzi.
Deo aliendelea na kibarua chake cha kuzungusha kiuno chake kwa tahadhari huku akianza kuhisi vitu vinatembea kwa mwendo wa kasi ya ajabu,kasi ikazidi kukolea na Leila akazidi kuongeza kukinyonga kiuno.
“Ah ah De..o aaah aaaah”
Leila alivyofika mlima kitonga akatulia.
***
Alivyojigusa chini baada ya kukurupuka kutoka kitandani asubuhi ya saa moja alikuwa amejichafua,ilikuwa ni ndoto nyevu.Hiyo ilimaanisha ushindi ni wake sababu mganga alimwambia kwamba akimuota Deo wanafanya mapenzi ndotoni ilimaanisha dawa zake zingefanya kazi endapo angeenda ofisini kwake kupeana naye mkono.
“Ngoja niende leo,maana jana nilimkosa na juzi.Leo niende asubuhi sana”
Leila aliwaza kichwani na kujitoa kitandani ambapo aliingia bafuni na kujimwagia maji,akatoa kikopo cheusi kutoka kabatini na kuanza kupaka dawa alizopewa na mganga mikononi mwake zoezi hilo lilivyoisha akavaa nguo na viatu.
Akabeba mkoba wake mdogo mkononi alimaarufu kama kipima joto,taratibu akaanza kushusha ngazi ambapo alivyofika nje alikutana na taxi.
“Nipeleke Posta,pale kwa jana”
“Poa”
Dereva alimuelewa abiria wake sababu siku iliyopita alimpeleka posta,bado alikuwa ana kumbukumbu na eneo hilo ndiyo maana hakuhoji sana maswali.
****
Dakika sabini baadaye Leila alikuwa akishuka ndani ya taxi akamlipa dereva ujira wake na kunyoosha mpaka jengo lililokuwa na ofisi ya Deo.Moyoni mwake hakuelewa kama Deo angemsamehe ama la! sababu mara ya mwisho waligombana kutokana na kumfumania na mwanamke mwingine.Alivyokanyaga ndani wafanyakazi wote macho yalikuwa kwake.
“Samahani za asubuhi?”
Leila alitoa salamu kwa msichana mdogo wa makamo mrefu aliyekuwa mapokezi ndani ya kioo ambacho chini kilikuwa na tobo kubwa.
“Salama,nikusaidie nini?”
“Nimemkuta Deo”
“Ndio yupo”
“Naweza nikaonana naye?”
“Nimwambie nani?”
“Mwambie Leila”
“Okay”
Msichana wa mapokezi ingawa aliijuwa sura ya mwanamke huyu na alikumbuka kila kitu kilichotokea lakini hakuwa na hiyana sababu mambo ya bosi wake na Leila hayakumuhusu hata kidogo ndio maana akainua mkonga wa simu na kubonyeza namba fulani akasubiri kama sekunde mbili.
“Halloo bosi,kuna mgeni wako hapa.Jina lake Leila.Okay sawa”
Mkonga wa simu ukarudishwa chini,Leila akawa anasubiri jibu lake, alielewa kwamba alizuiwa kuingia ndani, kupitia sura ya sekretari alilijuwa hilo.
“Pita ndani”
Kauli hiyo ikamfanya Leila ashindwe kuelewa kwamba amesikia vibaya ama ni kweli.
“Amesema niingie?”
“Ndiyo,anakusubiri”
Mwendo aliotumia Leila ulikuwa wa haraka,akakunja kona na kuusukuma mlango wa Kioo ambapo alikumbana na sura ya Deo inamtizama kwa hasira.
“Deo naomba nisamehe”
Leila akajifanya mpole ghafla na aliongea maneno hayo akiwa amesimama wima kama mlingoti,tumbo lake kubwa lipo mbele.
“Samahani kwa niliyokufanyia,ni hasira za mimba”
Leila aliendelea kumsihi Deo amsamehe akasingizia mimba kama kigezo cha yeye kumfanyia fujo ofisini kwake.
“Kaa kwenye kiti hapo”
Hatimaye Deo akajibu huku akisonta kidole kwenye kiti kimoja wapo cha kukaa wageni.

Mapigo ya moyo ya Leila yalikuwa yakipiga kwa nguvu kama kitenesi kinachodunda,kibarua cha kumpa mkono wa kushoto Deo kilianza kuwa kigumu kwa upande wake,alihisi mkono wake ni mzito.Alitetemeka na alihisi amepatwa na joto la ghafla mwilini.
“Oh kumbe hatujasalimiana”
Mwishowe akajitoa kimasomaso akatoa mkono wake wa kushoto alioambiwa na mganga wa kienyeji ampe Deo kwa nia ya kuipumbaza akili yake.Deo akainua kichwa chake,akautizama mkono wa Leila kwa kama sekunde mbili.
“Mkono wa kulia una nini?”
Deo aliuliza kwa kuwa alikuwa mwenye haraka hakusubiri jibu nayeye akatoa mkono wake wa kushoto,hakuelewa kwamba anafanya kosa moja kubwa sana.Mikono yao ikakutana juu ya meza.
Sijui ni kitu gani lakini haikuwa hali ya kawaida,Deo alihisi kama kichwa chake kinauma hususani utosini, wakati akihisi maumivu hayo Leila alikuwa bado ameung’ang’ania mkono wake.
“Deo are you alright?”(Deo uko sawa)
Leila akauliza.
“Yah”
Hatimaye wakaachiana.

****
“Atakuwa amepatwa na nini?Kwani ndiyo tabia yake au?”
“Hapana Mama, ni leo tu.Lakini nadhani yupo njiani anakuja, juzi aliniambia kuwa leo atachelewa”
“Una uhakika mwanangu?”
“Ndiyo Mama”
Ulikuwa ni usiku wa saa saba,kila mtu alikuwa macho kumsubiri Deo sababu haikuwa kawaida yake kuchelewa kiasi hicho.Marietha alivyoulizwa alimkingia kifua mumewe sababu hakutaka maswala yake ya ndoa ayaanike wazi sababu haikuwa mara ya kwanza kwa Deo kuchelewa kurudi hiyo ilikuwa ni kama mara ya tatu.
Hata yeye alianza kuingiwa na wasiwasi sababu hata simu ya Deo haikuwa hewani,muda ulizidi kwenda ikafika saa tisa za usiku bado Deo hakuonekana nyumbani.
“Mwanangu atakuwa amepatwa na nini?”
Mama aliuliza kwa simanzi, kitu kilichomjia kichwani ilikuwa ni wenda Mwanaye amepata ajali ingawa hakutaka kulipa swala hilo kipaumbele,Eva ndiyo usiseme machozi yalianza kumlenga.
“Wifi,una uhakika?Umepiga simu ofisini kwao?”
“Hapana”
“Embu jaribu inawezekana akawa amepata matatizo”
“Niwapigie sasa hivi?”
Lilikuwa ni swali lililokuwa lenye jibu la waziwazi sababu mambo yalivyokuwa yametokea Deo alitakiwa kupigiwa simu dakika hiyohiyo.
“Wewe unataka upige saa ngapi labda?”
Mama Deo akajibu kwa mtindo wa swali tena kwa kufoka.Ilibidi Marietha achukuwe simu na kuanza kumuulizia mfanyakazi mmoja baada ya mwingine.Simu ya mwisho kutoka kwa Mwanamke aliyeitwa Ruth Edson ikamfanya moyo wake upige paa!ndani kwa ndani.
“Ndiyo alitoka na mwanamke mmoja hivi asubuhi yaa saa tano.Utakuwa unamjua,anaitwa Leila baada ya hapo hakurudi tena ofisini”
Ruth Edson alihitimisha mazungumzo yake akiwa upande wa pili na kukata simu.


Ilikuwa yapata saa tano na dakika kumi na mbili asubuhi ofisini kwa Deo,sekunde tano zilizopita nyuma alihisi kichwa chake kinavuta akaona kama nyotanyota mbele yake ni baada tu ya kupeana mkono wa kushoto na Leila ambao ulikuwa na dawa za kishirikina, hapo ndipo mambo yalipoanza kubadilika,alimtizama Leila kwa macho yasiyo ya kawaida kabisa.
“Deo upo sawa?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Mshirikina Leila,kwa usomi aliokuwa nao ungeambiwa kwamba anafanya vitu kama hivyo habadani ungebisha,Mwanamke kama yeye ambaye Mungu alimpa nguvu na kichwa kizuri darasani kwa wakati kama huo angetakiwa kuwa ofisini ama katika majukumu ya ujenzi wa taifa na sio kushiriki mambo kama hayo ya kichawi na kugombania mapenzi.
“Deo,Talk to me”(Deo ongea namimi)
Akasema tena baada ya kumuona Deo ameganda kama barafu anayatumbua macho yake mbele ameganda kama barafu,akapitisha mkono mbele ya macho yake ili kama kumshtua lakini Deo alikuwa bado ameganda kama mstimu.
“Deo,Deo..”
Leila akaanza kumtingisha, hapo ndipo Deo aliposhtuka na kumtizama.
“Vipi Marietha,Sorry Leila..Kumbe umekuja muda sana”
“Nipo muda kweli”
“Kichwa changu hakipo sawa kabisa”
“Twende ukapumzike”
“Usijali”
“No please,standup”(Hapana,tafadhali simama)
“Leila No”
“Nakuomba,utamalizia kazi hizi kesho”
Leila akasimama kutoka katika kiti alichokaa na kuzunguka upande aliokuwa ameketi Deo akamshika mkono na kumuinua,hapo hakuwa na kipingamizi ingawa alikuwa ana uwezo wa kuweka mgomo lakini hakuelewa ilikuwaje mpaka akasimama kama mwanakondoo!
Akabeba simu zake wakatoka nje ambapo mlangoni alikumbana na Msaidizi wake mwingine aliyefahamika kwa jina la Ruth Edson huyu alikuwa katika kitengo cha uhasibu.
“Bosi kuna cheki hapa siielewi”
Ruth Edson alikuwa amesimama wima anamuangalia bosi wake kwa adabu zote, mkononi alikuwa ameshika hundi iliyomchanganya sababu tarakimu na maandishi havikurandana ndiyo maana hakuielewa sawasawa ilikuwa ni lazima aombe msaada kwa mkuu wake wa kazi kabla ya kuipeleka popote.
“Naomba niletee baadaye, sasa hivi natoka”
“Bosi,inahitajika sasa hivi”
“Leila! Sorry Ruth nimekuelewa”
“Hapa nimeshindwa kuelewa ina…”
“Ruth nimekwambia baadaye”
Deo akaongea kwa ukali na kupita kando yake,nyuma yake akifuatwa na Leila wanaongozana ambapo walitoka mpaka nje,huko ndipo Deo alipoingia ndani ya gari na kuondoka zake,akiacha kazi nyingi ofisini kwake.
“Tunaenda wapi?”
Deo aliuliza baada ya kuwasha gari,hakuelewa ni wapi anaenda.
“Landmark Hotel”
“Kuna nini?”
“Wewe twende”
“Aya”
Kitendo cha Deo kujibu hivyo alichukulia huo ni ushindi tosha,kwa upande wake alielewa tayari kwamba juju lake limefanya kazi.Deo aliendesha gari mpaka Landmark hotel hapo walishuka na kuingia ndani hotelini,chumbani.Deo akaketi juu ya sofa.
“Kaa kitandani”
“Usijali hapa panatosha,hujaniambia kwanini tupo hapa”
Badala ya Leila kujibu akamsogelea mpaka juu ya sofa na kumkalia juu ya miguu yake,akamgeukia na kumshika shingo akatoa ulimi wake akaanza kulamba ‘lips’ za Deo mkono wake wa kushoto akaupitisha mpaka kwenye zipu ya Deo na kuanza kupapasa kirungu,hapo ndipo Deo bila kusema chochote akaanza kuonesha ushirikiano.Akatanua mdomo wake ulimi wa Leila ukapenya ndani wakaanza kulana denda!
“Darling”
Leila akaita kimahaba huku macho yake yakiwa yamelegea.
“Yes My love”
“Nakupenda”
Deo hakujibu hapohapo akamvuta Leila tena midomoni mithili ya njiwa,Leila akasimama na kupiga magoti ambapo alitoa mkanda wa Deo akavuta suruali yake chini akamtoa nyoka ambaye alikuwa amesimama tayari,akamuweka mdomoni.Hakutofautishwa na mtu anayelamba koni,hapo ndipo Deo alipoanza kuchanganyikiwa.Alihisi kuna vitu vinatembea ndani ya mishipa yake ya damu,kazi yake ikawa ni kukishika kichwa cha Leila akiwa anakikandamiza juu ya nyoka wake.
“Aaaaah aaaah”
Hiyo ndiyo ilikuwa miguno ya Deo ya ndani kwa ndani,raha alizokuwa anahisi zilizidi kipimo chake.Akahisi nyoka wake kama ameingizwa ndani ya kitu chenye joto kali.Kuishi sana Uingereza kulimfanya aijue michezo hiyo ya kikubwa mbali na hapo Leila alikuwa hodari wa kuangalia sinema za ‘porno’ama ngono! Kama ungechukuwa simu yake na kuingia kwenye video zake basi asilimia themanini na tano ungekumbana na sinema hizo.Alihangaika na nyoka wa Deo sio kawaida mdomoni alijaza mate akazidi kumsugua,mpaka alipohisi vitu kama utomvu vimeanza kutoka,alishaelewa nini maana yake,akazidi kumlamba nyoka zaidi na zaidi.Hapo ndipo Macho ya Deo yalipoanza kubadilika rangi vitu kama utitiri vilianza kutembea kwa kasi akamshika Leila vizuri kwa nia ya kumtoa lakini Leila hakutaka kitu hicho kitokee,kufumba na kufumbua majimaji mazito kama maziwa vikaruka kama risasi mengine yakaingia mdomoni kwa Leila na mengine yakamchafua vibaya sana kifuani,hapohapo Deo akatulia.
“Sorry”
Deo akasema kwa uchovu.
Deo hakukumbuka tena kwamba alikuwa ni mme wa mtu badala yake alitoka juu ya kochi na kuvua nguo zake ambapo aliingia bafuni kujimwagia maji,alikuwa kama yupo nyumbani kwake vile na baada ya hapo akapita kitandani na kujitupa,hiyo ilimfanya Leila atabasamu akajiona yeye ni bingwa.
“Hapa kazi tayari kilichobaki ni kuingia ndani ya nyumba na kuwa mama mwenye nyumba,bila kupoteza muda”
Leila akaongea huku akilishika tumbo lake kubwa,mwanaume aliyelala juu ya kitanda ndiye alikuwa baba wa mtoto aliyekuwa tumboni kwake lilikuwa wazi kabisa sababu ndiyo huyu mwanaume aliyefanya naye ngono zembe yaani pekupeku!Ilikuwa furaha sana ndani ya mtima wake,akajiona yeye ndio yeye.
****
Alizinduka saa tatu ya usiku akiwa yupo kitandani bado,pembeni yake alikuwa amelala Leila anachezea simu akavuta kumbukumbu zake ni wapi alipo ingawa zilikaa sawa na kugundua kwamba hayupo nyumbani kwake lakini alipuuzia hakujishughulisha na hilo swala na wala hakujali,akajiona yupo sehemu sahihi kabisa.
“Kumbe nimelala sana eeh”
Akajifanya kuuliza ili kumshtua Leila.
“Lala tu usijali,au ngoja nikuletee wine”
“Poa”
Deo na Leila wakaanza kunywa pombe kali na kilichofuata hapo ni kutomasana katika miili yao,wakajikuta wanaingia tena kwenye tendo la kuzini.Deo alijikuta anampenda Leila ghafla bila kuelewa ni kwanini hali hiyo imejitokeza.
“Nataka niende nyumbani Leila,ngoja nikapumzike huko”
“Kwani hapa sio nyumbani?”
“Ni nyumbani lakini Mama yangu yupo unajuwa,akiondoka nitakuwa nakuja kulala hapa”
“Mimi na Mama yako nani zaidi?”
“Wote ni zaidi”
“Haiwezekani wote tukawa zaidi,chagua kimoja mimi au Mama yako”
“wewe Leila,Wewe hapo lakini naomba tu ruksa”
Sijui iliezeke vipi lakini Deo alikuwa ni kama zezeta ama mtu aliyelishwa limbwata.Hakuwa Deo wa kipindi cha nyuma mwenye kushikilia misimamo.
“Sawa nenda”
Leila akatingisha kibiriti akijifanya kama amesusa.
“Umekasirika?”
“Hapana,nakuruhusu uwende lakini kwa sharti moja”
“Lipi hilo?”
“Nataka hiii wiki niwe nimehamia kwako,nataka niishi nawewe”
“Ah Leila bado mapema sana,sasa na hiyo mimba itakuwaje?”
“Hii usijali”
Bado Leila hakutaka kutumbua jipu mapema kwamba Mimba aliyobeba niya Deo alitaka kwa wakati huo iwe siri kwanza.
Ilivyotimu saa nane Deo alivaa nguo zake na kumpiga busu Leila la kumuaga.
“Baby”
“Yes please”
“Simu yako”
“Uliizima?”
“Ndiyo sikupenda watu wakusumbue”
“Okay shukrani,nitakuona kesho”
Deo akabeba na funguo zake za gari akatoka nje huku nyuma akimuacha Leila anatabasamu,alikuwa ni mwanamke mwenye furaha kwani alianza kupiga picha jinsi atakavyoingia ndani ya jumba la Deo na kuishi naye kama mke na mme,hakujali watu wangemchukuliaje.
****
“Piii piiiiiiiiiiii”
Mlio wa honi uliwashtua Marietha na Mama Deo wakiwa na Eveline seblen.Wote wakafungua mlango na kutoka nje ambapo walishuhudia Mlinzi anafungua geti,gari la Deo likaingia ndani,taa zikazimwa Deo akashuka.
“Ulikuwa wapi?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Mama yake mzazi akiwa ametanda mbele yake,sura yake ilichora makunyanzi kitendo cha Deo kuchelewa kurudi kilimkera ingawa alikuwa mwenye wasiwasi kabla.
“Nakuuliza wewe Deo ulikuwa wapi?”
Mama Deo akauliza tena,safari hii aliuliza kwa sauti iliyosindikizwa na ukali.
“Mama shikamoo naomba nikapumzike ndani nimech…..paaaa paaaaaa”
Vilikuwa ni vibao viwili vya shavu,kimoja kilitua upande wa kulia hakukaa vizuri akapigwa kingine kushoto.Mama huyu alikuwa ana mkono mwepesi kitendo cha Deo kuanza kumjibu kitu tofauti na swali lake kilimfanya ajawe na ghadhabu.Marietha alikuwa pembeni machozi yanamlenga.
“Lakini Mama haipasw…”
“Nawewe kelele”
Eveline alivyotaka kuingilia akatulizwa na jicho kali alilokatwa na mama yake.
“Nakuuliza wewe Deo ulikuwa wapi?”
Mama Deo akarudia kuuliza swali lake.
“Kwenye msiba Mama”
Akadanganya huku akiwa mwenye hofu tena kwa sauti ya upole.
“Msibaaaaa?Msiba gani usitoe taarifa?”
“Samahani kwa hilo”
Baada ya kutoa jibu hilo alitembea na kunyoosha mpaka chumbani ambapo alijitupa kitandani,Marietha nayeye akaingia chumbani lakini alimkuta Deo alishauchapa usingizi hakuelewa amelala kweli ama la alielewa mumewe hakuwa msibani taarifa za kutoka ofisini na Leila ndizo zilimuumiza.Licha ya yote lakini hakutaka kumsumbua alichoshukuru ni Mumewe kurudi nyumbani,akabadili nguo na kuvaa za kulalia kisha kupanda kitandani.
***
Deo alibadilika kwa kiasi cha kutosha,tabia hiyo ilianza ghafla wakati mwingine alikata mguu kabisa hakutokea nyumbani hata kwa siku mbili.Kwa Marietha kuishi na Deo ilikuwa ni sawa na kukata kitunguu sababu alikuwa ni mtu wa kulia tu,hata Deo ikitokea amerudi nyumbani basi alikuwa akimtukana vibaya sana na kuondoka dakika hiyohiyo.
“Mwanangu”
Siku hiyo Mama Deo alimuita Mkwewe,tabia za Deo hata yeye zilimuogopesha hali hiyo ilimfanya ahisi kuna kitu ambacho hakikuwa cha kawaida kinaendelea.
“Ab..e ab..ee Ma…ma”
“Futa machozi usilie”
Mama alikuwa ndiyo kama amemwambia Marietha alie kwa sauti,Eveline alijawa na huruma alishindwa kuzuia machozi yake.Alimuhurumia mwanamke mwenzake, kitendo cha kinyama alichokuwa anakifanya kaka yake wa damu kilikidhiri na kuvuka mipaka tena kwa Mwanamke mjamzito.
“Njoo seblen tuongee”
Wote wakafika Seblen, Marietha akaketi juu ya sofa huku akiendelea kububujikwa na machozi.
“Niambie ukweli hivi ndivyo mlivyokuwa mnaishi kwenye ndoa?”
“Ha..pana Maaa..ma”
“Niambie ukweli”
Ikachukuwa kama dakika moja nzima mpaka Marietha kutulia,akamtizama Mama yake mkwe.Hakuelewa aanzie wapi kumuadithia mbali na hapo kuna kitu kingine kilimwambia anyamaze tu.
“Maama nampend…a sana Deo”
“Naelewa mwanangu ndiyo maana mpaka leo upo hapa.Niambie ukweli mimi ni Mama yake usinifiche”
Marietha akavuta kamasi na kuwatizama Mama yake mkwe pamoja na Wifi yake Eveline ambaye tayari alianza kububujikwa na machozi,wote walimsikitikia.

Kabla ya kuanza kuongea chochote walihisi geti la nje linafunguliwa na muungurumo wa gari unaingia,hakuna mtu aliyejiuliza ni nani sababu ilifahamika ni Deo lakini kilichowashtua zaidi ni kumsikia Deo anazungumza na mtu mwingine.
Hazikupita hata dakika mbili mlango wa Seblen ukafunguliwa,Deo alikuwa ametanda mlangoni na mabegi mawili ya nguo,jambo hilo likazuwa kitendawili kikubwa sana.Nyuma yake akatokeza Mwanamke mwingine mwenye tumbo kubwa la mimba.Marietha akaangua kilio kwa sauti kubwa sababu alimjuwa mwanamke huyo, sura hiyo haikuwahi kumtoka.
“Leila karibu nyumbani”
Bila kuwa na mshipa wa aibu Deo alitamka maneno hayo mbele ya Mama yake mzazi tena akiwa na Marietha pamoja na dada yake Eveline!




Kwa Marietha alilifananisha swala hilo na ndoto ya kuogopesha tena ya asubuhi.Mama Deo pamoja na Eveline walichukulia jambo hilo ni kama kiini macho na halikuwa kweli kabisa.Haikuwezekana hata kidogo kwa Deo kuingia ndani ya nyumba na mwanamke mwingine akiwa kushoto kwake tena akiwa mjamzito,picha waliyoitafsiri moja kwa moja ni kwamba Deo alikuwa akilala nje kwasababu ya mwanamke aliyekuwepo naye pembeni yake.Kazi ya Mama Deo ilikuwa ni kumkagua Leila kuanzia juu mpaka chini bila kum-maliza,akamgeukia mwanaye Deo.
“Wewe Deo huyu ni nani?”
Mama akatupa swali.
“Huyu Mama ni mkweo”
Bila kukwepesha wala kupepesa macho yake Deo alitoa jibu bila kuogopa chochote.Jibu la Deo lilikuwa kama mkuki wenye moto ukatua ndani ya mtima wa Marietha,nguvu zilimuishia akaangua kilio kama mtu aliyefiwa na wazazi wake wote wawili.
“Wewe Deo,Wewe Deooo”
“Naaam Mama”
“Huyo ndiye alikuwa anakufanya uwe unachelewa kurudi na kumuacha mkeo?Kwa taarifa yako hapa hakai”
“Mama,naomba tukapumzike tafadhali”
“Unasema nini?”
“Mama umenisikia”
“Mwanangu Deo embu nitizame Mama yako,unataka kuwa kama Baba yako?”
“Mama naomba tupite basi”
Tangu amzae Deo hakuwahi kupandishiwa sauti namna hiyo,jambo hilo lilimfanya ashindwe kuelewa ni kitu gani kilimpata mwanaye,bado hakuamini.
“Wewe mwanamke unanifahamu vizuri?”
Ilibidi Mama mzazi amgeukie Leila kwa macho makali ya hasira sababu alijuwa huyo ndiye chanzo cha yote kutokea, kama Mama ilibidi aingilie kati.Jinsi Leila alivyomuangalia Mama Deo ilitisha,alimpandisha juu mpaka chini na kubinua mdomo, hakutofautishwa na mtu aliyeona kinyesi ama kinyaa,hiyo ilikuwa ni dharau kubwa mno kwa mama huyu mtu mzima,jambo hilo lilishuhudiwa na kila mtu,Marietha,Eveline hata na Deo vilevile.
“Sina shida ya kukujuwa,muulize Mwanao”
Hilo ndilo jibu alilotoa Leila,Mama akapandisha mori akachomoka kama Mkuki ili kuimvaa Leila amtie makofi lakini Deo alimuwahi na kumshika.
“Mama embu nisikilize kwa umakini,naomba usitake kunifanyia fujo ndani ya nyumba yangu.Okay”
Japokuwa jambo la Mama yake kudhalilishwa aliliona lakini hakujali, alikuwa upande wa Leila kumaanisha kwamba kile alichokifanya kwa Mama yake kilikuwa sahihi kabisa.
Eveline aliyekuwa pembeni hakuamini hata kidogo kwa kitu alichokiona,akajipiga kofi la shavu ili kushtuka ndotoni lakini wapi, jambo alilokuwa analiona lilikuwa la kweli wala hakuwa ndotoni huyu ndiye alikuwa kaka yake wa damu aliyesomeshwa na mama yake kwa shida leo hii anafanya matendo ya kinyama,ilikuwa ni sawa na shukrani ya punda!
“Deo”
“Mama,naomba uwe mstaarabu”
“Baby nimechoka,chumba cha kupumzika kiko wapi?”
Leila akauliza kwa sauti iliyojaa huba huku akimnyali Mama Deo kwa njia ya kumpandisha juu mpaka chini,swali hilo alimuuliza Deo huku akimsogelea karibu na kumshika kiuno,akamtizama Marietha na kutoa msonyo mrefu.
“Twende chumbani”
Deo akamvuta Leila.
“Eveline nisaidie mabegi ya wifi yako kupeleka chumbani”
Eveline hakuwahi kuchukizwa kama siku hiyo,ni sawa alikuwa ni kaka yake wa kuzaliwa tumbo moja lakini kwa jambo alilolifanya lilivuka mipaka.Kauli aliyotoa Deo ilikuwa ni kama ameamsha mashetani yake,akamkata jicho baya Deo la chuki, machozi ya hasira yalikuwa yapo machoni tayari.
Alikuwa akihema,kifua chake kilikuwa kinapanda juu na kushuka,mapafu yake yakajaa hewa.Hakuwa mwenye nguvu za kumpiga Deo lakini alitamani afanye hivyo,alikuwa ana majibu mengi ya kumpa Deo kwa wakati mmoja lakini alishindwa kutamka sababu ya hasira kumkaba kohoni hiyo ikafanya mpaka midomo yake kumcheza.
“Any way”
Deo hakujali chochote alichofanya ni kumkokota Leila chumbani,mbaya zaidi kilikuwa ni chumba alichokuwa analala yeye na mke wake wa ndoa, Marietha! Hiyo ilimaanisha kwamba hatoshiriki na mke wake chumba kimoja tena, kuanzia siku hiyo.
“Pumzika hapa,ninarudi sasa hivi”
“Okay baby”
Leila alijiona bingwa kuliko mwanamke yoyote yule duniani,akatabasamu na kuanza kukagua chumba cha Deo kilivyokuwa kikubwa mno.Mbele yake aliona televisheni kubwa sana na chumba kilikuwa kisafi tena cha kisasa, kwa upande wake hakuamini kama tayari amemnasa Deo,shukrani zake zote alizipeleka kwa Mganga wake wa kienyeji.
“Yule Mganga kiboko,nitamlipa mara mbili yake”
***
“Marietha Mama usijali,nitaongea na mwanangu kila kitu kitakuwa sawa”
Mama Deo alipata kibarua cha kum-bembeleza Mkwewe Marietha,Eveline alikuwa juu ya sofa analia machozi ya hasira tu,kitu alichofanya kaka yake bado alishindwa kukifananisha na kitu chochote kile, ulikuwa ni zaidi ya unyama na kilichomshangaza ni kitendo cha kumjibu nyodo mama yake mzazi,hayo ndiyo mambo yaliyokuwa yanapita kichwani mwake na yalimuumiza mtima.
“Mh! Mh! Mh! Mh!”
Deo alivyoweka mguu wake Seblen aliguna kidogo huku akiwatizama ndugu zake,macho yake yalivyotua kwa Marietha akayashusha mpaka juu ya tumbo lililokuwa kubwa la mimba,kisha kupeleka macho kwa Mama yake.
“Mama na Dada yangu Eveline.Sasa hivi kuna utaratibu mpya,uongozi umebadilika.Nyumba yangu ni kama serikali,awamu ya tatu imepita sasa hii ni awamu ya nne.Naomba nifupishe ili tuokoe muda, jambo lililotokea ni maamuzi yangu binafsi sitaki niingiliwe,kama mtu atashindwa kuishi hapa anaweza akaenda tu”
Kwa Deo siku hiyo alijifananisha na Rais anayetoa hotuba kwa wananchi wake, kitu alichokuwa anakifanya alijiona yupo sahihi kabisa ndiyo maana aliongea bila wasiwasi.
“Oh,sijamaliza wewe wewe nani sijui Marietha,chumba chako kina mtu sasa hivi kwahiyo utafanya ustaarabu wa kutafuta chumba kingine ama utachukuwa maamuzi mengine.Sihitaji maswali,ahsanteni kwa kunisikiliza”
Huyu ndiye alikuwa Deo ambaye alikuwa anampenda Mkewe Marietha kuliko kitu chochote kile na hakuna hata mtu mmoja aliyemlazimisha kumuoa,leo hii amebadilika ghafla!Hakuna mtu yoyote aliyekuwa tayari kuamini kwamba Deo amebadilika kiasi hicho nyuma ya yote hayo waliamini kuwa mwanamke aliyemleta ndani ndiye chanzo cha yote.
“De…o kwe..li umea..mua kuni..fanyia hi..vi.Kwa..nin.i lakin..i? ungesubi..ri japo nijifungue”
Yalikuwa ni maneno kutoka kwa Marietha,aliongea huku akimwaga machozi na kwikwi ilimbana vibaya sana,maneno ya Deo yalikuwa magumu kupita moja kwa moja ndani ya moyo wake.Bado hakuamini kama huyu aliyesimama mbele yake ni mumewe wa ndoa waliyofunga kanisani.
Wakati mwingine alihusisha swala hilo na kizizi ama ndumba, wazo hilo lilivyomjia akalitupa mbali sababu katika maisha yake hakuamini ushirikina au nguvu za giza hata kidogo,ni kweli na haikuwa uwongo kwamba Deo alikuwa amebadilika, tena ghafla.
“Nimeeleweka nimesema kwamba,ni uamuzi wako kuishi hapa ama kuondoka.Chagua vilevile”
Wakati Deo anatoa jibu hilo Mama yake mzazi alichomoka na kunyoosha mpaka chumbani ambapo alitoka na mabegi yake ya nguo,akaburuza mpaka seblen.
“Mama unaenda wapi?”
Eveline akauliza.
“Ameshindwa kuishi mwache aende,nawewe ukitaka fuatana naye”
Deo akadakia kabla ya Mama yake kujibu,Eveline hakuwa nala kufanya nayeye akaingia chumbani akabeba kilichokuwa chake akatokeza seblen.
“Deo Mwanangu,mimi ni Mama yako.Nimekuzaa umekaa tumboni kwangu miezi tisa,nimekusomesha kwa shida Baba yako alivyoniacha,nimeuza senene pekupeku ili wewe usome”
Mama aliongea kwa uchungu!
“Kwani mama mimi nimekufukuza?”
“Hapana hujanifukuza mwanangu,mimi naondoka.Lakini naomba nikwambie kitu hiko kimoja,UTAKUJA BUKOBA HUKU UMENIPIGIA MAGOTI UNALIA MACHOZI”
“Mama mbona hivyo?”
“Nasema hivi,UTAKUJA BUKOBA HUKU UMENIPIGIA MAGOTI UNALIA MACHOZI”
Mama Deo aliirudia kauli hiyo kwa msisitizo sana akimwambia mwanaye.
“Mwanangu Marietha,ubaki salama Mungu atakupigania.Hizi ni changamoto ipo siku zitaisha”
Marietha alikuwa akilia bado, alitamani nayeye kuungana nao lakini hakutaka kufanya hivyo kwanza,alitaka kuzungumza na Deo faragha.
Hatimaye Mama Deo na Eveline wakafungua mlango na kutoka nje.
“Kwahiyo Mama mnaondoka?”
Jinsi Deo alivyouliza swali hilo wala hakumaanisha sababu alitumia sauti ya chini na aliuliza mara moja,kama angetaka ndugu zake wabaki angetilia swala hilo mkazo, hiyo ilimaanisha kwamba alifurahi na aliona kwamba atakuwa huru atajiachia na Leila wake,hakuelewa kwamba kwa kufanya hivyo ni sawa na kuukumbatia mzinga wa nyuki,hakuelewa kwamba amekaribisha pepo ndani kwake na siku yoyote litamnyonya damu!
“Mama lete nikusaidie hili begi”
Eveline alisema walivyofika getini akabeba begi la Mama yake.
Mama Deo akasimama na kujifunga kanga vizuri akamgeukia mwanaye Deo aliyekuwa kibarazani, wakatizamana kwa kama sekunde tano nzima bila kum-maliza hata kidogo.
“Aya Mama twende,sasa hivi tutapata basi kweli?”
“Ndiyo tutapata,nitapanda hata lori la mizigo ili mradi tufike mwanangu”
Ilikuwa ni picha ya kuuzunisha, haikuwezekana hata siku moja kwa mtoto kumfanyia unyama mama yake kama huo,Deo alimtizama mama yake pamoja na mdogo wake Eveline,wakafungua geti na kutoka zao nje.
“Funga hilo geti na kufuli”
Deo alitoa amri hiyo kwa mlinzi wake wa getini kisha kurudi ndani.
“Deo”
Seblen alikumbana na Marietha.
“Sema”
“Nimekufanya nini mme wangu?”
“Hujanifanya chochote naomba nikapumzike”
Deo akajibu kwa mkato,akatembea mpaka chumbani na kuubamiza mlango, kabaaa!

*****
“Katrina nisikilize”
“Nani akusikilize?Siwezi kukusikiliza Hemed.Nimekuvumilia nimechoka kabisa bora nibaki mwenyewe”
“Huko unafika mbali mpenzi wangu”
“Acha iwe hivyo”
“Katrinaa Katrinaaaa”
Sio siri ungekuwepo pembeni ungedhani watu hawa wawili wanafanya maigizo kumbe ilikuwa ni ukweli kabisa kwamba Mwanaume aliyekuwa akibembeleza alitolewa nje, ilionekana kuwa watu hao walikuwa wapenzi na leo hii ndiyo ulikuwa mwisho wao.
Katrina alikuwa ni msichana mrembo aliyekuwa ana asili ya kihindi lakini maisha yake alikulia sana barani Afrika nchini Tanzania sababu huko ndipo yalikuwa makazi ya wazazi wake,alikuwa ni mtoto wa kipekee kutoka katika familia ya kitajiri na kitu kilichomfanya atengane na wazazi wake siku zote ni masomo,wazazi wake waliamua kumpeleka nchini India kwa ajili ya masomo yake ya chuo kikuu,huko ndipo alipokutana na Hemed wakajikuta wanaingia katika mahusiano ya kimapenzi.
Ni kweli alijuwa anafanya makosa makubwa sana kutembea kimapenzi na Mwanaume wa kiafrika jambo ambalo baba yake alikuwa akilipiga vita,wahindi walikuwa wabaguzi kupita kiasi na siku zote hawakutaka mabinti zao waolewe na mtu yoyote mwenye ngozi nyeusi,wakiita ngozi ambayo iliyolaaniwa.
“Katrina vipi?Mbona unalia?”
Alivyofika hostel akakumbana na rafiki yake anayelala naye chumba kimoja yaani ‘roommate’huyu aliitwa Kajol alikuwa ni muhindi mwenzake.
Alivyomuona rafiki yake analia ikabidi amsogelee karibu ili amuulize.
“Hemed”
“Hemed kafanya nini?kakupiga?”
“Ha..pa..na amenitenda nimemkuta na Carol wananyonyana midomo yao”
“Sio kweli”
“Hu..niamini au?”
Kuanzia hapo kilichosikika kilikuwa ni kilio kutoka kwa Katrina na alilia kwa uchungu sana,maumivu aliyosikia moyoni yalikuwa ya namna yake.
Tangu azaliwe hakupata maumivu kama siku hiyo, akaamini maumivu ya mapenzi ni zaidi ya msiba.
Alichoshukuru ni kwamba Hemed hakuwahi kuiona nguo yake ya ndani ingawa alijipa moyo lakini bado alihisi moyo wake unamuuma,alikuwa ni binti mdogo mwenye umri wa miaka ishirini tu,katika chuo hiko kikuu cha Mumbai ndiye aliyetingisha kwa uzuri,alikuwa ana midomo midogo pua nyembamba iliyojichonga na nywele ndefu za singasinga ambazo mara nyingi hupenda kuzibana kwa nyuma.
Ilibaki miezi miwili tu ili wafanye mitihani ya kumaliza muhula, hivyo ilimaanisha kwamba alitakiwa kuwa jasiri.Ni kweli Hemed hakuacha kumsumbua,kazi yake ilikuwa ni kumuandikia barua za msamaha na kumsimamisha kila alipomuona.
“Katrina”
“Nini lakini?Mbona unakuwa hunielewi siwezi kuwa na wewe Hemed tafadhali tusikerane niache nisome”
“Bado nakupenda,naomba unisamehe”
“Kaendelee na Carol”
Hapo Hemed hakuwa na hoja yoyote ile,alibaki kumtizama Katrina kwa macho ya majuto kupita kiasi.
“Lak…”
Kabla ya Hemed kumalizia anachotaka kusema Katrina akasimama kutoka kitini na kuondoka zake,hiyo ilimaanisha hakutakiwa.
***
Siku hazigandi! Kadri siku zilivyozidi kwenda mbele ndipo Katrina alianza kumsahau Hemed taratibu sababu alijishughulisha na maswala yake ya kimasomo,hatimaye mitihani ikaanza na baada ya siku saba wakamaliza.Chuo hiko cha Mumbai kilikuwa kina ratiba ya mwaka mzima hivyo mkononi alikuwa ana tiketi tayari sababu alivyotoka Tanzania alikatiwa ‘Go and return’ yaani kwenda na kurudi.
Chuo kilivyofungwa hakutaka kupoteza wakati akafungasha virago vyake na kwenda kulala hotelin ili kesho yake apande ndege arudi nchini Tanzania,Katrina aliipenda sana nchi ya Tanzania ingawa alikuwa ana asili ya kihindi ndiyo maana muda wote moyo wake ulikuwa una dunda kwa kihoro.Na kwa wakati huo muda wote alikuwa kwenye kompyuta yake ndogo ana ongea na wazazi wake kwa njia ya skype.
“Ulale mapema,kesho usije ukachelewa ndege”
“Hapana Mama,ndege ni saa nane mchana”
“Sawa Mwanangu,masomo vipi?”
“Yanaenda vizuri japo magumu kiasi”
“Mimi na Baba yako tunakusubiri”
Katrina na wazazi wake walikuwa wanaongea huku wanaonana kwenye mtandao.Na siku ya siku ilipofika Katrina alikuwa njiani anaelekea uwanja wa ndege.
***
Ilikuwa ni furaha iliyozidi kifani ndani ya familia ya dokta Kapoor na Mkewe Khaila baada ya mtoto wao wa kipekee kurejea nchini Tanzania akitokea masomoni India,wakiwa ndani ya gari Katrina aliwaelezea wazazi wake jinsi mambo yalivyoenda, alivyofika siku ya kwanza jijini Mumbai na akahitimisha kwamba amezoea tayari mazingira na masomo yalikwenda vizuri kabisa.
“Ndio Mama vipi nyumbani anti Wahida hajambo?”
“Yupo,anakusubiri kwa hamu sana lakini leo ametoka”
Mpaka wanafika nyumbani nje ya geti kubwa bado Katrina alikuwa anaongea tu.Geti lilivyofunguliwa aliona mabadiliko makubwa sana nyumbani kwao,nyumba ilipakwa rangi nzuri na kulikuwa na bustani nzuri ya maua kwa pembeni.Wakashuka ndani ya gari na moja kwa moja akachomoka na kuingia ndani,ambapo alikimbilia juu ya sofa akakamata rimoti ya luninga na kuwasha.
“Kabadilishe hata nguo basi,alafu punguza sauti ndani kuna mgonjwa”
Baba yake mzazi alitoa maagizo hayo na kupita ndani ambapo alimuacha Katrina ameduwaa,Mama yake alivyopita akamsimamisha.
“Maaa”
“Vipi?”
“Nasikia kuna mgonjwa ndani?Ni nani?”
“Ndio,kuna mgonjwa punguza sauti tafadhali”
“Ni nani?”
Aliuliza na kukwapua rimoti pembeni ambapo alianza kupunguza sauti hapohapo,akamgeukia mama yake.
“Nani anaumwa mama?”
“Ni stori ndefu kidogo”
“Yuko wapi?”
Katrina aliibuka na maswali mengi sana na alitaka kujuwa mgonjwa huyo ni nani hususani,Mama yake hakuwa na kipingamizi.Wakatembea mpaka chumba cha tatu kutoka seblen,mlango ukafunguliwa.
Katrina na Mama yake wakazama ndani,ambapo walikumbana na kitanda, juu amelala mwanaume anapumulia mtungi wa hewa ya oxygen pembeni kuna mashine nyingine za mapigo ya moyo.
“ANAITWA ISSA”
Mama alisema!
****

Maisha ya Marietha yalikuwa magumu mno kuanzia siku hiyo Leila alivyoingia ndani ya nyumba,alivumilia akawa analala chumba kingine. Kila kukicha alikuwa mtu wa kulia na wakati mwingine Deo hakumpa pesa yoyote ile ya kutumia mbali na hapo kuna siku alishinda njaa bila kuweka hata kitu chochote mdomoni,Deo alifanya hivyo sababu kauli hiyo ilitoka kwa Leila, hakujali kwamba Marietha ni mkewe wa ndoa na isitoshe walikula kiapo kanisani,kwa Marietha ndoa yake tayari iligeuka na kuwa Jehanam!
“Wewe Malaya,embu amka”
Marietha alikurupushwa kitandani na maji ya baridi,alikuwa ni Leila akiwa ameshika ndoo iliyokuwa na maji asubuhi ya saa kumi na mbili.
“Unalala nini?Unalala nini?Kwanza inabidi leo uondoke hapa.Subiri uone”
Leila alitoka chumba anacholala Marietha,akatembea mpaka chumba wanacholala yeye na Deo.
“Deo,wewe Deo…Deoo”
Deo alikuwa akiamshwa tena kwa kuvutwavutwa,Leila hakutumia ustaarabu hata kidogo.
“Nini sasa,unataka nini?”
Kutokana na uchovu kitendo hiko kilikuwa kama kero kwake.
“Amka amka”
“Kuna nini?”
“Wewe nimekwambia amka”
“Alafu tusikerane,niache nilale”
“Unasemajeee Deo?”
Leila akauliza kwa ukali akiwa ameshika kiuno,hiyo ilimfanya Deo aogope kidogo!
“Una shida gani?”
“Njoo huku,Mkeo kanitukana”
“Kakwambia nini?”
“Deo inuka basi”
Akatoka kitandani akiwa na uchovu wa hali ya juu akiwa na bukta tu.Wakaongozana mpaka chumba alichokuwa analala Marietha.
“Wewe Marietha,ndiyo nini?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Deo tena kwa ukali wa hali ya juu,macho yake yalikuwa mekundu na kitendo cha Leila kumkurupusha asubuhi alikijumuisha humohumo ikawa tafrani!
“Nakuuliza wewe mbwa,ndiyo nini kumtukana Leila?”
Lilikuwa ni tusi kubwa kwa Marietha tena lenye uzito kufananishwa na mnyama mbwa,machozi yalianza kumtoka.
“Deo Mu…me wa..ngu nini la..kini?”
Marietha alijikaza akiongea kwa kwikwi.
“Nini kilikufanya umtukane Mpenzi wangu?”
“Mimi sija..fanya hivy…o ye..ye ndiyo ame…kuja kunimwa..gia maji”
“Mwongo mkubwa”
Leila akadakia.
“Baby,mimi sitaki kumuona hapa ndani huyu mwanamke wako.Kama unanipenda mtoe hapa”
“Wacha abaki hapahapa”
“No,nimesema sitaki kumuona.UMENISIKIA”
Leila akaongea kwa ukali na kumfokea Deo.
“Marietha,pack your things and leave”(Marietha chukua kilicho chako uwende)
Deo aliongea kwa kumaanisha na kumkata jicho kali Marietha,Leila aliachia tabasamu, kwake ulikuwa kama ushindi.
“Baby kwani hapa alikuja na nini?Nina amini hakuja na chochote,anaweza kuondoka hivyohivyo”
Leila akazidi kuchochea.
“Marietha ondoka sasa hivi,sitaki kukuona hapa.Fanya haraka.Ninaingia ndani,nikitoka nisikuone hapa nyumbani kwangu”
“La…kini De…o mi…”
“Nimemaliza,sitaki kurudia tena”
“Hutakiwi si uwende ebooo,macho yale kama vidonda”
Leila akasindikiza kwa matusi,akaondoka na kumuacha Marietha analia machozi.

Dakika tano nzima aliendelea kububujikwa na machozi ya uchungu,mlango ukafunguliwa Deo akaingia, safari hii mkononi alikuwa ameshika mkanda.
“Nilikwambiaje?Nakuuliza nilikwambiaje?”
Deo aliuliza kwa ukali huku akiuviringisha mkanda vizuri mkononi mwake,kama paka mwitu akamvaa Marietha na kuanza kumchalaza mikanda ya kichwa na tumboni.Kipigo alichokuwa anampiga hakikutofautishwa na Mwanajeshi anayempiga mwizi sababu alimvuta kutoka kitandani na kumtupa chini sakafuni akaanza kumshambulia na mateke ya tumbo.
“Nimekwambia uondoke hutaki malaya wewe, sasa leo ninakuuwa”
Deo aliendelea kumpiga mkewe wa ndoa,Leila nayeye akatokeza wakaanza kumchangia na mbaya zaidi Leila alikuwa akimpiga Marietha tumboni ili aiharibu mimba.
Marietha alikuwa akilia machozi ya uchungu na baada ya dakika tatu alikuwa akivuja damu puani na mdomoni,mwili wake karibia wote ukawa umevulia damu, hata hivyo kipigo kiliendelea tu!

ILIPOTOKA
Ndoa ya Marietha imevurugika kuwa tamu mpaka shubiri ni kitu kimoja tu,Nguvu za giza ambapo Mwanamke Leila anamuendea Mume wake kwa mganga kisha anaibuka kinara.Ilikuwa ni kama sinema vile kumbe ni kweli,akili ya Deo ilichukuliwa yote akawa ana buruzwa kama gari bovu.Ndoa ikazidi kuwa chungu zaidi baada ya Mwanamke Leila alipofanikiwa kuingia ndani ya nyumba, hiyo ilipelekea mpaka Deo amfukuze Mama yake mzazi pamoja na mdogo wake Eveline,wakaondoka wakimuachia laana kubwa.Hakuishia hapo,alianza kumtesa mkewe wa ndoa akishirikiana na Leila.Siku hiyo asubuhi na mapema wakamshambulia kama mpira wa kona!
SONGA NAYO.

Kilio cha Marietha kilisikika mpaka nyumba za jirani na wa kwanza kusikia alikuwa mlinzi wa getini lakini hakuwa ana uhakika kama kelele hizo zilitokea ndani ya nyumba anayolinda,akatega sikio vizuri.
“Huyo sio Mama?kuna nini tena?”
Mlinzi alijiuliza mwenyewe maswali bila kupata majibu ya haraka,akaanza kusogea taratibu, hapo ndipo alipojuwa kwamba ndani kuna purukushani na Marietha alikuwa akipigwa,aliisikia vizuri sana sauti ya tajiri yake Deo ikitamka maneno yaliyomshtua sana.
“Leo nina kuuuwa”
Kipigo kiliendelea,Marietha alikuwa amepasuka vibaya sana usoni, Deo alivyoona haitoshi akazungusha mkanda akawa ameushika kwa upande wa pili yaani upande wa ‘bacon’ kwenye chuma.Kwa nguvu akampiga nao Marietha kichwani, damu zikaruka mithili ya bomba la maji lililotobolewa.Kuanzia hapo hazikusikika tena kelele za aina yoyote ile Marietha alikuwa chini kimnya amelala,hasemi wala hajitingishi isipokuwa damu zilikuwa zinamtoka usoni na kichwani mithili ya sufuria linalovuja mchuzi jikoni.Jambo hilo lilimfanya Deo asitishe zoezi lake,Leila akarudi nyuma hatua kumi.
“Deo umeua!”
Leila alisema kwa hofu ingawa walikuwa wakimshambulia Marietha pamoja, alisema hivyo ili kujitoa kwenye msala,aliogopa kwenda kuozea gerezani.
“Deo Mungu wangu umeua”
Leila akazidi kusisitiza na hivyo ndivyo ilivyokuwa.
“Bosi”
Mlinzi wa getini nayeye akatokea kwa nyuma,alivyoona tukio hilo alipigwa na butwaa la waziwazi hasa macho yake alivyoyatupa chini na kumuona Marietha amelala damu zinamvuja,zimetapakaa chini.Kufumba na kufumbua wakaanza kusikia kelele nje za majirani,Deo aliweza kuitambua sauti ya Mr.Okama jirani yake, mkurugenzi wa shirika la umeme Tanesco, Ubungo.
“Jamani humo ndani kuna nini?”
Sauti ya Mwanamama mmoja ikasikika ikitokea nje,hii ilikuwa ya Mama Tunu,sauti hizo zote Deo alizijua.Akatoka nje haraka.
“Mr.Okama ninaomba msaada wako tafadhali”
Umri wa Deo na Mr.Okama ulikuwa unafananafanana, walikuwa wenye makamo sawa,walivyofika ndani cha Kwanza Mr.Okama alianza kuhoji.
“Nini kimetokea?”
“Okama nisaidie kummbeba tumuwaishe hospitali,mshike huko miguuni.Leila niletee funguo za Verosa juu mezani pale”
Deo alikuwa kama mtu aliyechanganyikiwa,akamshika Marietha kichwani huku Okama akiwa ameshika upande wa miguu, wakam-beba msobemsobe wakaanza kumtoa nje,kabla hawajafika kwenye gari Leila alitoka nje akiwa na funguo mkononi mwake,Marietha akaingizwa ndani ya gari na safari ikaanza papohapo.

Deo alikimbiza gari kama mtu aliyerukwa na akili,alikuwa mwenye wasiwasi mithili ya mtu anayeoga nje,ndiyo maana hata akasahau kuvaa suruali,alikuwa na bukta tu tena bila shati.
“Deo nini kimetokea?”
Mr.Okama alianza kumsaili Deo lakini hakujibiwa chochote,badala yake Deo alizidi kuendesha gari mpaka walipofika hospitali ya Kimara, wakashuka na kuomba msaada kwa wauguzi!
***
Marietha alitundikiwa dripu tatu za maji zote zikaisha, akawekewa ya nne ndipo alipoanza kupata nguvu sababu ya maji hayo kuchanganywa na Glucose,mbele yake alimuona Mama yake mzazi akilia machozi,kulia alimuona Deo Karekezi mikono yake yote ameikusanya kifuani kama mtu anayesali,macho yake yalikuwa mekundu na sura yake ilikumbwa na majuto makubwa,alimtizama mkewe akashindwa kujuwa aanzie wapi.
“Mariethaaa”
Deo aliita akaanza kusogea karibu lakini Marietha aligeuza shingo upande wa pili,bado picha ya kupigwa ilimjia kichwani mbali na hapo bado alikuwa anahisi maumivu makali ya kichwa na tumbo.
“Marietha,naomba unisamehee mke wangu.Nipo chini ya miguu yako”
Marietha aliyasikia vizuri sana maneno ya mume wake lakini badala yake alihisi uchungu ajabu,akaanza kumwaga machozi yakachuluzika pembeni ya macho yakaanza kulowanisha mashuka,hakuna mtu yoyote aliyegundua hilo isipokuwa kwikwi ndiyo ikafanya watambue kwamba Marietha analia.
“Marietha”
Deo akaita na kumshika.
“Niacheee,Deo niacheeee ondoka sitaki kukuona”
Mkono wa Deo ukatupwa mbali na Marietha aliongea kwa sauti kubwa ya hasira hiyo ilifanya dripu iliyochomekwa mkononi kwenye mshipa ichomoke.
“Samahanini naomba mtoke nje kidogo”
Kwa kasi ya umeme muuguzi akatokeza baada ya kusikia kelele kutoka kwa mgonjwa wake.
“Lakini ni mke wangu”
“Sawa kaka,lakini naomba umuache mgonjwa apumzike”
Sio Deo aliyetolewa nje hata mama Marietha vilevile,wote wakasimama varandani.
“Baba kwani nini kimetokea?”
Mama Marietha akauliza kwa unyonge ingawa alisikia fununu kwamba mwanaye alipigwa kipigo cha mbwa mwizi.
“Mama ni mambo tu ya kawaida”
“Kama umemchoka mwanangu tafadhali Baba,bora uniambie arudi kwangu”
Alitamani kuweka jambo hilo kifuani lakini alishindwa,Mama alishikwa na uchungu wa uzazi hali ya mwanaye ilimtisha mno,kilichomuuma zaidi ni ujauzito aliobeba Marietha.
Mpaka wakati huo bado alidhani yupo kwenye njozi sababu isingewezekana hata kidogo kwa mtu kama Deo kumpiga mkewe kiasi cha mpaka kutaka kumuuwa.
“Mama, lakini naomba hayo mambo tuzungumze baadaye”
Deo alihisi aibu,hata yeye alishindwa kuelewa ni shetani gani alimkumba mpaka akampiga mkewe wa ndoa.
Walikaa hospitalini mpaka saa kumi na mbili ya jioni,vipimo vilionesha kwamba hali ya Marietha ilikuwa mbaya lakini mtoto bado yupo hai,hilo likamfanya Deo ashushe pumzi nzito.
“Ahsante sana dokta”
Ni kweli Deo tangu asubuhi hakurudi nyumbani hiyo ilimpelekea mpaka akanunua nguo nyingine sababu alitoka nusu uchi nyumbani kwake.

***
“Sawa mimi nitatayarisha chakula baby”
“Si bora nikanunue tu”
“Hapana,wacha nipike nenda kaoge ubadilishe nguo,uwahi”
Lilikuwa ni kosa kubwa tena la Jinai kumuachia Leila apike chakula cha Marietha ili Deo akipeleke hospitali kwani aliweka dawa kali za kuharibu mimba aliyotoa kwa mganga wa kienyeji,hiyo ndiyo nafasi ya pekee aliyokuwa anaisubiri kwa hali na mali.
Baada ya dakika kumi akawa amerost ndizi tayari akachukuwa kipande cha nyama ya bundi alichopewa na mganga wa kienyeji aweke kwenye chakula.Akachanganya kwenye nyama ya ng’ombe, haikuwa kazi rahisi kwa mtu yoyote yule kugundua kwa macho ya kawaida.
Akafunga vizuri kwenye 'hotpot' na kuweka mezani, seblen.
“Hiko chakula tayari?”
Deo aliuliza baada ya kutoka chumbani.
“Ndiyo kipo mezani hapo”
Chakula kilikuwa mezani kimefunikiwa vizuri,kabla ya kukibeba akafungua ili kukagua ni aina gani ya chakula.
“Ahsante Leila,Maji kwenye friji yapo?”
“Ndiyo,yapo”
Deo akanyoosha mpaka kwenye friji akafungua na kuchukuwa chupa moja ya maji ya Kilimanjaro,akaweka ndani ya mfuko na kutumbukiza 'hotpot' ndani yake.Hakuelewa kwa kufanya hivyo ilikuwa ni jambo la hatari sana na alikuwa akienda kumuuwa mtoto wake mwenyewe,akatoka nje akaingia ndani ya gari na kutokomea nje ya geti.
“Kazi imeisha,utakuwa tasa maisha yako yote”
Leila alisema huku akitabasamu.

***
Deo aliwasiri hospitalini akiwa na mfuko mweusi wenye chakula kilichowekwa dawa na Leila ili mimba ya mkewe iharibike na awe mgumba maishani mwake,hakujua lolote yeye alijuwa wenda Leila alikuwa akijipendekeza ili makali ya kesi yapungue sababu ilikuwa ni kosa kubwa kisheria kumpiga mwanamke mjamzito.Alivyofika mlango wa wodi alilolazwa Marietha akashusha pumzi kidogo na kusukuma mlango,alimkuta Marietha yuko peke yake,akapiga hatua kadhaa mpaka kitandani kwake.
“Nimekuletea chakula”
Deo akasema lakini Marietha alimtizama bila kumjibu chochote.
“Kuna ndizi na nyama,kaa ule”
Deo akajisemesha tena ingawa alijuwa Marietha alimsikia,akaanza kutoa ‘hotpot’ ndani ya mfuko na kuweka pembeni juu ya meza ndogo.
“Nimeshiba,Ahsante”
“Basi japo kido…”
“Deo nimekwambia nimeshiba,huelewi Kiswahili?Hata kama ningekuwa nina njaa kiasi gani,siwezi kula chakula chako hata siku moja.Naona unataka kuja kunimaliza kabisa hospitalini,kama uliweza kunipiga kiasi kile hutoshindwa kuniwekea sumu”
Marietha aliongea kwa sauti ya ukali na mwisho akahitimisha kwamba Deo aondoke kwani anazidi kumfanya azidi kuumwa.Aliendelea kupiga kelele mpaka wauguzi walipotokea wakamtoa Deo nje,alivyotaka kuingia alizuiwa na kuambiwa kwamba asionekane hospitali mpaka hali ya mgonjwa itakapotengamaa.
“Basi nisaidie kitu kimoja nesi”
“Kitu gani?”
“Mpatie hiki chakula japo ale”
“Sawa”
Deo akakabidhi chakula na kutoka nje,akaingia ndani ya gari. Kabla ya kuliwasha akaegemea usukani akili yake ilikuwa imevurugika kwa kiasi cha kutosha.Akainua kichwa chake kiuvivu na kuwasha gari ambapo safari ya kwanza ilikuwa ni nyumbani kwake,alikuwa amechoka akili mpaka mwili.
****
Breki ya kwanza ilikuwa nyumbani kwake,akafunguliwa geti na mlinzi na kuingiza gari ndani,akaliweka vizuri kwenye maegesho na kushuka,akagonga mlango.
“Naniiiii?”
Sauti iliyotokea ndani ndiyo ilisikika, alikuwa ni Leila.
“Deo”
“I’m coming”(Nakuja)
Baada ya dakika moja mlango ukafunguliwa.
“Chakula alikula?”
Hilo ndilo lilikuwa swali la kwanza kutoka kwa Leila.
“Hajala,naomba kupita”
“Unasemaaaa?Kwanini hajala?”
“Leila nipishe bwana nipite.Nimechoka sana”
Deo alishindwa kuingia ndani sababu Leila alikuwa ametanda mlangoni,mikono kaitandaza huku na kule.Ulikuwa tayari usiku umeingia,Deo alihisi kuchoka na alitaka kupumzika mbali na hapo alikuwa na ‘stress’ kichwani,kukaa kwa Leila mlangoni aliona ni kama kupotezewa wakati.Alivyotaka kutumia nguvu,Leila akamzuia.
“Leila nipishe basi,siko vizuri”
“Nikupishe uende wapi?rudi ulipotoka”Swala la Marietha kutokula chakula ndilo lilimchanganya!
Na Kilichowafanya waache malumbano ni baada ya simu ya Deo kuanza kuita na alivyoitoa kutoka mfukoni aliona jina Dokta Adela,simu hiyo alijuwa ilitoka hospitali aliyolazwa mkewe,Marietha.
Akaipokea na kuiweka sikioni.
“Habari dokta”
“Salama tu,njoo hospitali mara moja”
“Kuna nini Dokta?”
Deo aliuliza akiwa mwenye wasiwasi,Leila alivyoona hivyo nayeye akasogea karibu na sikio la Deo lenye simu ili asikilize kinachotaka kuzungumzwa.
“Kuna tatizo limetokea,mkeo amezidiwa sana”
“Kivipi?Wakati nimetoka hapo akiwa katika hali nzuri”
“Hata mimi nashindwa kuelewa,lakini ni baada ya kula chakula”
“Whaaaat”(Niniiiii)
“Ndio nakuomba mara moja,alafu kuna kitu unatakiwa ukijuwe”
“Kitu gani daktari?”


Kila alipokumbuka kipigo alichopigwa na mume wake alibaki akilia tu,alikuwa juu ya kitanda cha wagonjwa anaugulia maumivu bado,usoni alikuwa na bandeji na pembeni kulia kwake kulikuwa na dripu yenye Glucose inayopitisha maji hayo kupitia mshipa wake wa damu uliopo mkononi.Kila lililotokea katika maisha yake bado hakuamini kama ni kweli,akachukuwa muda kidogo na kurudisha kumbukumbu zake nyuma,akamuona Issa walivyokuwa wanaishi kwa furaha na amani tele ingawa alikuwa maskini,alitamani mambo yarudi nyuma angalau arekebishe mambo yaliyotokea lakini haikuwezekana sababu muda hauwezi kurudi nyuma kamwe,vitu vilivyotokea vikawa kama historia.
Alikumbuka vitu vingi mno,pia alimkumbuka Deo baada ya ndoa na misukosuko aliyokuwa anakumbana nayo, kifupi Marietha siku hiyo alikuwa kama mtu anayetizama filamu ya kuuzunisha ndiyo maana akawa anamwaga machozi ya uchungu.
“Marietha”
Sauti hiyo ndiyo iliyomzindua kutoka kwenye dimbwi la mawazo,alikuwa ni mama yake mzazi anaweka vyombo juu ya meza ndogo iliyokuwa pembeni yake.
“Chakula nimekuletea”
“Ahsante Mama”
“Unajisikiaje sasa hivi?”
“Hivyo hivyo,kichwa na mbavu bado vinauma”
“Pole mwanangu,washakuja kukuona wauguzi?”
“Ndio”
“Alafu nimepishana na Deo nje”
“Chakula gani umeniletea?”
Marietha hakutaka kusikia habari za Deo ndiyo maana akapindisha mada.
“Wali na kuku na Juisi”
“Ahsante nitakula”
Mama alijisikia uchungu ajabu!Alitamani kuongea kitu lakini alishindwa,alimuonea mwanaye huruma.
“Vipi dada,unajisikiaje?”
Nesi aliingilia maongezi yao,baada ya kumfikia mgonjwa wake,Marietha.
“Vizuri tu”
“Kuna chakula hapa,nilipewa na Mumeo”
“Ahsante nimeshiba”
“Kula japo kidogo”
“Mama angu ameniletea chakula”
“Aya”
Hakukuwa na namna tena nyingine ya kumlazimisha Marietha ale chakula, alichofanya muuguzi ni kukiweka juu ya meza ya Marietha kisha kuondoka zake.
“Amka ule mwanangu,upate nguvu”
Akatii amri akakaa kitako na kufungua chakula alicholetewa na mama yake mzazi na kuanza kula.
“Naomba Maji Mama”
Baada ya kupiga kijiko cha tatu akashushia na maji makubwa ya Kilimanjaro,akaendelea kula tena.Katika hali isiyo ya kawaida alianza kuhisi tumbo linamuuma, kwa mara ya kwanza alidhani wenda ni kawaida lakini kadri sekunde zilivyozidi kwenda mbele ndipo kichomi kilizidi kumshika,akashindwa hata kuweka kijiko kilichokuwa na chakula mdomoni.
“Vipi?!”
Mama akauliza kwa hamaki.
“Tumbo”
“Marietha,Mariethaaa”
Kuendelea kubaki kuliita jina la mwanaye bila kuita msaada wowote ilikuwa ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu,Mama Marietha akakimbia akitoka nje ya wodi huku akipiga kelele kama mwehu mpaka kwa daktari,akamvaa na kumkwida koti.
“Nini?”
“Mwanaaanguuu”
Dokta alishindwa kuelewa,koti lake lilikuwa linavutwa alimanusura lichanwe.
“Mama utanichania koti langu,una shida gani?”
“Mwanangu anakufa”
“Yuko wapi?”
Dokta akaungana na Mama Marietha,wakanyoosha mpaka wodi alilolazwa Marietha ambapo walimkuta amejikunja ameshika tumbo lake.
Kilichotokea ni kuwekwa haraka kwenye machela,ikasukumizwa mpaka kwenye chumba kingine kwa ajili ya vipimo mbadala.
***
Deo alikuwa njiani anaendesha gari,msongamano wa magari ndiyo uliyofanya achukie zaidi,Moyo wake ulikuwa ukipiga kwa nguvu mithili ya kitenesi sakafuni.Alitamani kupaa angani ili aikwepe foleni,dakika arobaini nzima alikuwa kwenye msongamano,akaona isiwe tabu.Akageuza shingo yake nyuma ili aangalie nafasi arudi nyuma kisha atanue aweke gari kando aangalie ustaarabu mwingine lakini alishindwa sababu nyuma kulikuwa na gari lingine tena karibu tu,ikabidi ashuke na kutembea mpaka kwenye gari hilo aina ya IST nyeusi yenye vioo vyeusi pia yaani tinted,akagonga kioo.Kikashushwa sura ya mwanamke wa kihindi ikatokeza akiwa amevaa miwani ya macho.
“Samahani unaweza kurudisha gari yako nyuma kidogo,nataka nipite pembeni”
“Sasa mimi rudi nyuma vipi?siwezi rudi nyuma acha kusumbua mimi”
Alikuwa ni dokta Khaila akielekea nyumbani kwake,pembeni alikuwa na binti yake Katrina,yeye hakuwa na habari yoyote alikuwa ameshika simu anachat.
“Kuna nafasi huku nyuma”
“Acha kusumbua watu”
Hatimaye kioo kikapandishwa juu.
Deo hakuwa na jinsi ilibidi arudi ndani ya gari lake asubiri gari zisogee.Dakika kumi baadaye gari za mbele zikaanza kutembea, alichofanya ni kupita pembeni baada ya kupata upenyo, akaweka gari kando na kushuka.
“Psiiii bodaaa”Akaita.
Pikipiki iliyokuwa inapita pembeni yake ikapiga msele na kusimama.
“Nipeleke hapo hospitali ya Minja,bei gani?”
“Buku nne”
“Poa”
Deo akapanda nyuma ya pikipiki safari ya kwenda hospitali ikaanza,dakika kadhaa baadaye akawa amefika, akatoa noti ya shilingi elfu tano bila kudai chenji akanyoosha mpaka ndani hospitalini,ulikuwa ni usiku mnene.
“Samahani mimi naitwa Deo Karekezi...Mama Mama”

Kabla ya kumalizana na Mwanamke wa mapokezi mbele yake alimuona Mama Marietha amesimama ukutani analia machozi,akajikongoja na kumsogelea.Kuna kitu alijifunza kupitia uso wa Mama huyu,hakukuwa na habari njema,ndiyo maana akasogea kiminyato.
“Mama”
Mama Marietha alikuwa ameegemea ukuta hakuelewa ni kitu gani akifanye,Marietha alikuwa ameingizwa ndani ya wodi lingine huku akilalamika kwamba tumbo linamuuma,kivyovyote vile kulikua na habari mbaya tena za kutisha.
“Samahani,njoo ofisini”
Mwanamama aliyevaa koti jeupe alimuita Deo ofisini kwake.
“Keti”
Deo akakaa kitini baada ya kufika na alikuwa mwenye wasiwasi.
“Kuna nini daktari?”
Deo alitupa swali lakini badala ya kujibiwa Dokta Adela alimkata jicho kali sana,kupigwa kwa mwanamke mwenzake kulimfanya akasirike, habari hizo alizijua sababu Marietha alibanwa na kusema kila kitu.
“Mkeo ana hali mbaya,nini kimetokea?”
Dokta Adela akauliza lakini alikuwa akijuwa ukweli wote.
“Ali ali li ali alidondoka kwenye ngazi,akaumia vipi hali yake kwa sasa?Dokta kuna nini?”
“Angalia huyu mpumbavu ananidanganya,wanaume wengine sijui wapoje”
Dokta Adela aliwaza huku akiwa bado anasikiliza talanta za Deo.
Siku zote mtu akikudanganya kwa maneno nawewe mdanganye kwa kumsikiliza sababu Kila kilichozungumzwa aliitikia, kazi yake ilikuwa ni kutibu wagonjwa sio kuwafanyia upelelezi ndiyo maana akapiga kimnya.
“Kuna vitu hapa,mkeo alikuwa hapati lishe bora hivi karibuni isitoshe mtoto amekaa vibaya tumboni,pia ana UTI hii ni mbaya sana inaweza kupelekea mimba kuharibika,ninachokuomba hata tukimruhusu kesho usifanye vitu ambavyo vitampa Stress,make sure anakula vizuri,anahudhuria clinic”
Habari hizo kwa Deo zilikuwa mbaya upande fulani lakini nzuri vilevile sababu mambo aliyokuwa anawaza yalikuwa ni tofauti.
****
Alikataa katukatu kurudi nyumbani hivyo alivyoruhusiwa aliamua kuishi kwa Mama yake ili apate amani ya moyo aliamini huko atakuwa salama mpaka pale atakapojifungua mtoto,japokuwa alikuwa anapigiwa simu nyingi na kutumiwa meseji kutoka kwa Deo akitaka asamehewe lakini wapi, hakujibu wala kupokea simu zake!Haikuwa kazi rahisi hata kidogo kubadili mawazo yake,Marietha alichomoa na aliendelea kushikilia msimamo wake kwamba hatorudi kwa Deo tena, labda akishajifungua mtoto.
“LAKINI KOSA GANI LISILO SAMEHEWA MKE WANGU,NIMEKUZOEA TAFADHALI RUDI NYUMBANI.POKEA BASI HATA SIMU ZANGU ILI NIJUE HALI YAKO,SAMAHANI KWA YOTE”
Siku hiyo alikuwa juu ya kochi anasoma meseji simuni,nyingine ikaingia kabla ya kumalizia mlango ukagongwa,kwa uvivu akajiinua na kuuendea,akufungua.
“Shemeji”
Ilikuwa ni sura anayoifahamu kabisa wala haikuwahi kumtoka,Mwanaume aliyekuwa mbele yake alikuwa amepigilia suti nyeusi kohoni tai imemkaa sawasawa,alikuwa rafiki mkubwa wa Deo, bwana Ayambo.
“Karibu ndani shemeji”
Ingawa alijuwa kilichomleta Ayambo lakini hakutaka kuonesha chuki,bifu lake lilikuwa kati yake na Deo sio na Bwana Ayambo.
“Vipi hali Shemeji?”
“Salama tu,nikuletee nini?”
“Hapana shemeji,usijali nimekunywa chai tayari”
Mpaka hapo ukimnya ukatawala,Bwana Ayambo alikuwa akifikiria ni kwa namna gani aseme kilichomleta,akakohoa kidogo.
“Shemeji”Akaita.
“Abee”
“Unajuwa sisi ni watu wazima,na watu wazima siku zote hawagombani.Hata Malaika wa bwana huko mbiguni wanachukizwa.Bado Deo anakupenda sana na anahitaji urudi”
Marietha alimuacha Ayambo aongee kila kitu mpaka mwisho,alivyomaliza akatabasamu na kumtizama kwa umakini.
“Ndio alivyokutuma uje kuniambia?”
“Hapana shemeji”
“Hajakwambia kuwa ana mwanamke mwingine?”
“Mimi ninakujuwa wewe”
“Acha unafki,kama una mengine sema lakini kama kuhusu Deo tafadhali sitorudi na sitomsamehee”
Huo ndiyo ulikuwa msimamo wa mwanamke huyu Marietha,hakuelewa somo hata kidogo!
****
“Deo unasema nini?Huyu ni nani?”
“Wewe Mwanamke embu kuwa mstaarabu,sawa?”
“Kelele Malaya wewe”
Ndani ya DM Grocery kulikuwa na tafrani jioni ya saa kumi,Deo alikuwa katikati ya Leila na Olivia.Jinsi mambo yalivyoenda hakuweza kufungua kinywa chake kuongea chochote na hakuelewa akae upande gani sababu alikutwa na Olivia kwa mara nyingine.
“Nani Malaya?”
Olivia akauliza na kusimama wima,hasira zilikuwa kohoni mbali na hapo alikuwa mwanamke mtata hata Deo alilitambua hilo.
“Olivia tafadhali embu acha fujo”
Deo akaingilia ili kusawazisha mambo!
“Deo usinishike,tueshimiane tena tueshimiane na huyu mshirikina wako”
Kufumba na kufumbua watu wakaanza kujaa na kuwazunguka,Deo aliona aibu ajabu, kwa mtu mwenye heshima zake kama yeye kitu kama hiko kilikuwa ni kashfa kubwa.
“Nani mshirikina?”
Leila akauliza kwa hasira,ikawa kama ameguswa mshono,ukweli ulimuuma!
“Wewe ha……paaaaaa”
Ilikuwa ni sauti ya kibao na kilimuingia Olivia vizuri shavuni.Hakutaka kuendelea kuongea, nayeye akarusha kofi,mambo yakawa yameharibika tayari.Akashika chupa ya ‘Tusker light’ iliyokuwa mezani tena ina bia, akampiga nayo Leila kichwani pwaaa! Ikampasukia, damu zikaruka,Olivia hakuishia hapo akashika tena chupa nyingine ya konyagi akairusha ikamfikia Leila usoni puu,watu wakaanza kuingilia,wakawatenganisha.
“Niache nimuoneshe huyu Mchawi”
Olivia alitaka kujitoa katikati ya watu waliomshika!
“Jamani tunaomba njia,tumpeleke huyu Mama hospitali”
Leila alikuwa akivuja damu usoni anaingizwa ndani ya gari analia kama mtoto, ameshika tumbo lake lenye mimba,na kilichomuogopesha zaidi ni damu zilizokuwa zinamvuja katikati ya mapaja yake.



Moto aliouwasha ulikuwa mkali zaidi tena wa petrol, haukuwa rahisi kuuzima hata kwa maji,kwa upande wake hakutegemea kama mambo yangekuwa mazito namna hiyo,Leila alizungukwa na watu alikuwa amepigwa vibaya sana na chupa za uso, alihisi maumivu makali mno mbali na hapo alihisi kuna kitu kama maji vinavuja katikati ya mapaja yake,akajigusa taratibu akitumia kiganja chake, alivyotoa mkono alikumbana na damu hapo ndipo alipohisi uchungu ajabu!
“Mwacheni huyu Malaya nimuoneshe”
Kwa nguvu za ajabu Olivia aliwasukuma wanaume wawili waliokuwa wamemshika akakamata chupa nyingine ya Serengeti na kuirusha,ikawa bahati mbaya kwake na nzuri kwa Leila sababu chupa ilimkosakosa na kugonga kwenye verosa ya Deo,kioo kikatoa ufa.Olivia alikuwa mwanamke mtata.Wanaume wengine sita wakamshika na kumvuta.
“Wewe dada tulia basi,usituletee bangi hapa.Tutakuzaba makofi shauri yako, embu tulia mse** wewe”
Mwanaume mmoja aliongea kwa jazba.
“Weeee! weeee! mse** baba yako,tena ukome embu jaribu.Unanijua mimi ni nani,mbuzi pumbavu zako.Niachie mjinga wewe”
Olivia alizidi kuongea maneno makali,kwa mwili aliokuwa nao na maneno aliyokuwa anayotoa kinywani vilikuwa ni vitu viwili tofauti kwani mwanaume aliyekuwa amemshika alikuwa ni kipande cha mtu.
Kwa wakati huo Leila alishikwa na watu watatu na Deo alikuwa nyuma yake wakamuingiza mpaka ndani ya gari kwa safari ya kwenda hospitali kwa ajili ya matibabu.
“Funga mlango,funga mlango”
Deo alitamka akiwa nyuma ya usukani mlango wa gari ukafungwa, akatia gari moto na safari ya kuelekea hospitali kuanza mara moja.Ndani ya gari Leila alikuwa akijinyonga, tumbo lilikuwa linamuuma ajabu na alihisi kichomi cha kukata.
Damu nyingi ziliendelea kumchuluzika na alikuwa akipiga kelele za kufa mtu.
Kazi ya Deo ilikuwa ni kunyoosha mguu na kuyapita magari mengine, kelele zilivyozidi akanyoosha mkono na kukiweka kioo cha katikati sawa ili kumuangalia Leila aliyekuwa nyuma anapiga yowe,alichokiona kilimshtua,damu zilikuwa nyingi kwenye dera lake ilibidi ageuze shingo nyuma.
“Leilaaa”
“Deoo tumbooo”
Wanaume waliokuwa nyuma,wamekaa pembezoni mwa Leila walishaelewa nini maana yake,hisia za mimba kuharibika ndilo jibu lililowajia moja kwa moja na jambo hilo lilikuwa wazi kabisa kwamba Mimba ya Leila ilikuwa imetoka kwa asilimia tisini.Ndani ya dakika kumi na tano Deo alikuwa anaweka gari nje ya hospitali ya Ukonga iliyoitwa Miko hospital,wote wakashuka na kuomba msaada wa wauguzi.Manesi walitoka mkuku mkuku mpaka kwenye gari ambapo walisaidiana kumchukuwa Leila mpaka ndani kwa ajili ya matibabu.
Hakuna siku iliyomchanganya kama siku hiyo,kwanza alilia na kutoa kamasi nyepesi,mimba ya Leila ilikuwa imetoka na alihitajika kushonwa nyuzi tisa usoni kutokana na chupa alizopigwa nazo.
“Pole sana”
Dokta alijaribu kumfariji Deo lakini wapi.Uchungu na hasira vilimbana vyote kwa wakati mmoja,hapohapo akatoka nje na kutoa simu yake ya mkononi,akatafuta namba fulani na kuipa simu ‘ok’.
“Yes naongea na Kamanda Amata?”
“Ndio Deo za masiku”
Deo hakupoteza wakati,niya ya kumpigia simu Kaminsha wa jeshi la polisi kanda ya Ziwa Kamanda Amata ilikuwa ni kumuweka Olivia chini ya ulinzi kwa kitendo alichokifanya.
Hicho ndicho kitu kilichoenda kutokea,kwani baada ya dakika arobaini akarudishiwa jibu kwamba Olivia yupo chini ya ulinzi!
***
“Dolla ngapi?”
“Dolla elfu tatu na mia mbili”
“Ni ndogo ongeza bwana”
“Hapana,siwezi”
“Kama huwezi kuongeza siwezi kufanya kazi yako”
“Okay niongeze ngapi?”
“Dolla elfu tatu na mia tano,fanya hivyo”
“Hapana labda mia nne”
“Nimekwambia dola elfu tatu na mia tano,sipandi wala sishushi”
“Sawa,mzigo napata lini?”
“Nikipata mzigo wangu kazi itafanyika”
“Sawa kesho nitakuingizia kwenye akaunti yako,Napata ngapi?”
“Kumi”
“Sawa”
Yalikuwa ni mazungumzo ya simu ya mkononi tena kwa lugha ya kihindi.Dokta Kapoor alikuwa simuni anaongea na upande wa pili,jinsi alivyokuwa anaongea kwa wasiwasi ilionekana kabisa alikuwa akifanya mazungumzo haramu.Ni kweli hiyo ilikuwa wazi kwamba nyuma ya utajiri wa daktari huyu kuna mambo hatari alikuwa akifanya,kuuwa watu na kuuza figo za binadamu wenzake.Wakati mwingine aliwatoa figo moja bila kujuwa na kuuza,figo moja alikuwa akiuza zaidi ya shilingi milioni mbili za kitanzania.
Biashara hiyo ilimfanya atajirike kwa kasi ya ajabu, akafungua sheli za mafuta na hospitali nyingine nyingi ili iwe rahisi kwa biashara yake kukuwa,jina lake lilivuma kwa kasi ya kimbunga na lilikuwa zito sababu alikuwa ni daktari mzuri,kilichowapumbaza watu zaidi ni jinsi alivyokuwa ana moyo wa kujitolea,kila mwisho wa mwezi aliwatembelea watoto yatima na wagonjwa mbalimbali na kuwapa misaada wakati mwingine alikula nao pamoja,hakuna mtu yoyote aliyegundua kwamba Dokta Kapoor alikuwa ni chui aliyejifika ngozi ya mwanakondoo.
Siri hiyo ilikuwa nzito sababu hata mke wake hakujuwa lolote lile ingawa alilala naye chumba kimoja.Hakuna siku iliyomfurahisha kama alivyopokea simu ya dili la shilingi dola elfu tatu na mia tano za kimarekani kutoka kwa Abdulrahman huyu alikuwa muhindi mwezake lakini alikuwa mfanyabiashara mkubwa.
“Nina wagonjwa tisa hapa hospitali,bado mmoja nitamtoa wapi ili nikamilishe figo kumi”
Dokta Kapoor aliwaza kichwani mwake,figo tisa alikuwa nazo tayari,alihesabu idadi ya wagonjwa mahututi walioletwa hospitalini hivyo ilibidi mwenyewe awapasue na madakatri wenzake ambao humsaidia kufanya kazi hiyo haramu,hao aliwalipa mara mbili ya mshahara wa kazi hiyo ili kuwafunga midomo.
“Safi,moja nitatoa kwa Issa.Mambo tayari”
Hapohapo akasimama na kuvaa koti jeupe ambapo alinyoosha mpaka kwenye ofisi ya Dokta Kadir Raul,akamtonya na kumueleza shida yake.
“Sawa saa ngapi?”
Dokta Kadir Raul akauliza.
“Saa moja jioni,leo tutawapasua wagonjwa wote tisa.Nadhani itachukuwa muda kidogo.Dokta Amir Adam yuko wapi?”
“Anaingia shifti ya usiku”
“Sawa,anza kujiandaa”
Hakukuwa na muda wa kupoteza hata kidogo ilivyofika saa moja jioni, Dokta Kapoor na timu yake wakaingia thieta na makoti ya kijani huku pua zao zikiwa zimefunikwa na vitambaa maalum,ndani ya chumba hiko kulikua na mgonjwa aliyepata ajali mbaya ya gari hivyo alitakiwa kushonwa na kufanyiwa upasuaji.Lakini madaktari hawa walitaka kufanya kitu kingine hatari cha kumtoa figo moja na kuiweka ili baadaye wakauze.
Hicho ndicho kitu walichoanza kukifanya.Kwa utalaam waliokuwa nao kazi hiyo ilikuwa ni sawa na kuweka kikombe cha chai mdomoni,ndani ya dakika kumi walikuwa wametoa figo tayari.Wakaiweka pembeni na kumshona mgonjwa kisha wakaendelea kumfanyia matibabu mengine.Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa mgonjwa aliyefuatia,siku hiyo walifanya kazi hiyo mpaka saa nane za usiku,Thieta ilikuwa bize kupindukia.
“Tayari figo tisa”
Dokta Kapoor aliwaambia wenzake baada ya kuzihesabu,akaziweka ndani ya mashine ndogo maalum ili zisiharibike.
“Ahsanteni sana na poleni,wiki ijayo kila mmoja wenu nitampa dola mia saba”
“Ahsante bosi”
Dota Kapoor akawa wa kwanza kutoka thieta na boxi kubwa ambalo ndani lilikuwa na figo za binadamu,akaingia mpaka ofisini kwake na kuzihifadhi sehemu maalum,akatabasamu na kujifuta jasho.
Alivyochukuwa simu yake alikutana na ‘Missed calls’ nyingi kutoka kwa mkewe dokta Khaila,ikabidi ampigie.
“Mbona nakupigia simu hupokei?”Lilikuwa ni swali kutoka kwa Dokta Khaila.
“Nilikuwa thieta,leo nilikuwa nina wagonjwa wengi,vipi Katrina mshatoka kutembea?”
“Ndio muda mrefu,nilikuwa na wasiwasi”
“Ah mimi niko salama,hata hivyo ndio narudi nyumbani”
“Sawa nakusubiri”
“Okay”
Simu ilivyokatwa ikamuacha Dokta Kapoor anavua koti lake,akaweka kila kitu sawa na kubeba funguo zake za gari na safari ya kurudi nyumbani kwake kuanza mara moja.
Kichwani mwake alimfikiria Mgonjwa aliyeitwa Issa ilikuwa ni lazima amtoe figo moja ili figo kumi zikamilike apige pesa,Dokta Kapoor siku zote aliwaza pesa tu kuliko utu.
“Kweli akiba haiozi siku zote leo ndio nimeamini”
Dokta Kapoor alitamka methali hiyo akiwa ndani ya gari lake anarejea kwake!
****
Hali ya Issa iliendelea kuwa nzuri kadri siku zilivyozidi kwenda mbele sababu aliweza kuongea na kukaa kitandani bila kupata maumivu yoyote yale ya mgongo kama hapo awali,hiyo ilikuwa moja ya furaha kubwa kwa dokta Khaila sababu kila siku katika dua zake hakusahau kumuweka mgonjwa wake huyo katika maombi,jambo hilo kwake alilichukulia kama muujiza wa Mungu ndiyo maana akazidi kumuombea kwa Mungu tena na tena.
Mwanaye aliyeitwa Katrina alikuwa likizo na wote walisaidiana kuhakikisha Issa anapata matibabu vizuri mpaka afya yake inakuwa sawa.
“Vipi hali yako?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Dokta Khaila akitaka kujua afya ya Issa.
“Naendeleea vizuri tu”
“Kweli?”
Akauliza tena kana kwamba hana uhakika.
“Ndio”
Bado aliendelea kudhani yupo ndotoni bado hakutaka kuamini kwamba binadamu wenye roho kama hizo wapo duniani mbaya zaidi wenye asili ya kihindi.
Issa alichukuliwa kama mmoja wa wanafamilia na alipendwa,Dokta Kapoor na mkewe walivyotoka huku nyuma walimuacha Katrina akimuangalia Issa ambaye alimchukulia kama kaka yake.Kumpelekea chai,chakula cha mchana na matibabu kama dawa zilikuwa juu yake na Dokta Khaila aliporudi usiku aliwajibika na kumshughulikia Issa.
“Kaka Issa chakula”
Ilikuwa ni sauti nyororo kutoka kwa Katrina akiwa chumbani kwa Issa.
“Ahsante”
Mazoea ya Katrina na Issa yaliota mizizi na mwezi mmoja baadaye Issa alianza kufanya mazoezi ya kutembea,Katrina ndiye alikuwa akimfanyisha mazoezi na alijihisi mwenye furaha sababu hakuwa na mtu mwingine wa kuzungumza naye,walianza kuzoeana taratibu, siku moja alitaka kujua nini kilimkumba Issa mpaka akapata ajali mbaya.
Hakukuwa na sababu ya kuweka mambo kifuani,Issa akaanza kufunguka kila kitu kilichotokea katika maisha yake,hakubakisha hata kitu kimoja,akasimulia jinsi alivyompenda mwanamke anayeitwa Marietha na kumaliza na Katrina yeye akaanza kusimulia jinsi alivyotendwa kimapenzi,siku hiyo kwao ilikuwa ya uzuni sana.
Kutokana na majonzi wakajikuta wanakumbatiana kwa hisia kali,damu zao zikaanza kuwaenda mbio ajabu,ilikuwa ni kama shoti ya umeme ilikuwa imepita miilini mwao.Kufumba na kufumbua Katrina akavuta kidevu cha Issa akamvaa mdomoni wakaanza kubadilishana mate kwa njia ya ndimi jambo ambalo lilikuwa hatari sana na kama Dokta Kapoor angewakuta basi angem-meza Issa mzimamzima!
***
Mtoto huyu kisura hakuishia hapo alitaka makubwa na alifanya mambo ya hatari sana,siku hiyo usiku aliamka saa saba na kuingia chumbani kwa Issa akiwa na nguo ya kulalia peke yake,kuna kitu alikuwa anakihitaji ndio maana akafanya hivyo.Issa hakuwa anaelewa lolote alikuwa usingizini fofofo,alizoea kulala mapema na siku hiyo Dokta Kapoor alichelewa kurudi kutoka hospitali.
“Issaaa..Issaa..”
Katrina aliita na kuanza kumpapasa Issa mwilini mwake,hususani kifuani.
“Katri….”Issa akakurupuka hakuelewa kama yupo ndotoni au ni kweli.
“Shhssss shssss”
Issa akazibwa mdomo na kiganja cha Katrina ili asipige kelele,kufumba na kufumbua akapandiwa kwa juu,Katrina alikuwa ana mdomo mdogo na mlaini,akapanua mdomo wake na kutoa ulimi akautumbukiza kinywani mwa Issa,wakaanza kubadilishana mate.Kila sekunde zilipozidi kwenda mbele ndipo damu zao zilizidi kuchemka!


Haikuwa rahisi kwa Katrina kutoka juu ya kiuno cha Issa,alidhamiria kukidhi haja yake.Ukweli ni kwamba hakumjuwa mwanaume katika maisha yake wala hakuelewa ni ujasiri gani uliomkumba mpaka akaingia chumbani kwa Issa na kuanza kufanya mambo hayo ya uasherati.Siku zote ikishafikia hatua hiyo hakuna binadamu yoyote mwenye hisia kamili ambaye ataweza kuchukuwa maamuzi sahihi,Issa alijiona yupo sawa na ndiyo maana akapitisha mkono wake mpaka chini ya kitovu cha Katrina,akazidi kuudidimiza mpaka chini kwenye maporomoko, alivyotaka kuguza kibumbuna Katrina aliweka mkono wake sababu hakuwa tayari kuguswa eneo hilo mbali na hapo hakuna mwanaume yoyote aliyewahi kugusa sehemu zake nyeti na kama ingetokea Issa angefanya hivyo basi angekuwa wa kwanza,kifupi Katrina alikuwa msichana bikira ndiyo maana hata alivyokuwa anafanya tendo hilo majasho yalikuwa yakimtoka sababu alikuwa hajui ashike kipi aache kipi,alichohisi yeye ni raha za ajabu mwilini mwake,wakazidi kulana denda huku wakipapasana.kila Issa alipojaribu kupitisha mkono wake ndani ya ikulu ulizuiwa.Wakabilingishana kitandani,Issa akawa juu yake!Akapinjua kamba ya ‘night dress’ kifua cha Katrina kikabaki nje,Issa hakuchelewa akafakamia maziwa na kuanza kuyanyonya hiyo ndiyo ilimfanya Katrina apagawe zaidi,vitu vilivyokuwa vinatembea ndani ya mwili wake alishindwa kuvielewa, vilikuwa ni kama utitiri na vilianzia kutokea nyuma ya mgongo wake,vikapita kwenye nyonga na kuzidi kutembea.Wakati akisikilizia raha hizo Issa alikuwa tayari keshaitoa nguo yake bila yeye mwenyewe kujijua,akatoa mashine yake akaipanua miguu ya Katrina,akaweka mtambo sawa taratibu akaanza kuuzamisha ndani ya mgodi uliokuwa mdogo na mgumu.
“Ngo! Ngo! Ngo! Ngo!”
“Ngo! Ngo! Ngo! Ngoo!”
Wa kwanza kusikia mlango ukigongwa alikuwa ni Issa ingawa bado hakuwa mwenye uhakika kama ni kweli ama amesikia vibaya,akasitisha zoezi lake la kutaka kuingiza mashine ndani ya mgodi ili achimbe madini.Hiyo ilimfanya Katrina nayeye atulie kidogo sababu mlango ulianza kugongwa tena,kama wangepimwa mapigo yao ya moyo basi kipimo kingeonesha yanadunda mara mia saba kwa sekunde.Katrina alitetemeka na alionesha kuchanganyikiwa, hakuelewa ni kitu gani angesema endapo angekutwa na wazazi wake chumbani kwa Issa,kipigo kingemuhusu.Alimuelewa baba yake alivyokuwa mkali kama pilipili mbuzi!
“Ngo ngo ngo,Issa”
Moyo wa Katrina ukapiga paa!Ilikuwa ni sauti ya baba yake mzazi na katika kumbukumbu zake hakukumbuka kama alivyoingia ndani ya chumba hiko alifunga mlango na ufunguo,alitamani ageuke awe m-bu aruke lakini swala hilo halikuwezekana,kama mshale akaruka kutoka kitandani na kuingia bafuni, aliamini huko ndipo ingekuwa salama yake.
“Issaa…Issa..”
“Naaam..Naaaam”
“Wewe fanya nini?Umelala?”
Lakini katika kitu alichokizingatia mzee huyu katika maisha yake ni jambo moja tu ustaarabu, ingawa alikuwa katili lakini swala la ustaarabu kama lingekuwa na mtihani basi angefaulu kwa kupewa alama A+,kabla ya kuingia chumbani kwa Issa aligonga mlango japokuwa ilikuwa ni nyumba yake na kama angeingia siku hiyo bila kugonga na kumkuta mwanaye anafanya kitendo hicho,siku hiyo angemnyonga mtu kwa mikono yake.
“Hapana..Ndio”
Issa akapata kigugumizi.
“Nataka fanya mazungumzo nawewe,kuongea nawewe kesho subuhi”
“Sawa ha hahakuna shaka”
“Sawa lala salama”
Mpaka hapo ukimnya ukatawala,Issa hakuwa na uhakika kama Mzee Kapoor ameondoka au amejibanza mlangoni,alikuwa ana wasiwasi mwingi.Alivyopiga jicho pembeni akamuona Katrina katoa paji la uso anachungulia, hata yeye alikuwa mwenye hofu kuliko kawaida.
“Ameondokaa?”
Katrina akauliza kwa sauti ya chini huku akionesha hofu ya waziwazi.
“Ndio”
Issa akajibu, kilichofuata hapo ni Katrina kuanza kunyata mpaka mlangoni,akanyonga kitasa taratibu na kutoa kichwa chake nje kwa tahadhari,alikuwa kama mwanajeshi anayechungulia adui yake vitani.Alivyoona mambo yapo shwari bila kuaga akatoka, akatembea mpaka chumbani kwake na kujitupa kitandani, bado hakuamni kwamba amepona kwenye tundu la sindano!
****
Huduma kwa Marietha zilisitishwa tangu alipoondoka kutoka kwa mumewe baada ya kupigwa kipigo cha mbwa,hakupewa aina yoyote ile ya matunzo yaani pesa za matumizi,na Deo akamchunia mazima, hakutuma tena watu wam-bembeleze.
Kama mwanamke mjamzito alitakiwa kuudhuria kliniki lakini yeye alikuwa nyumbani kwa Mama yake anakula msoto.
Cha kusikitisha zaidi na pesa alizokuwa anatumiwa mama yake Marietha kutoka kwa Deo pia zilikata.Siku hiyo Mama Marietha alivyoenda kujaribu kwenda kuangalia akaunti yake benk CRDB Mnazi mmoja tawi la vijana akaambiwa kwamba akaunti ilikuwa imefungwa hivyo hakuweza kupakuwa pesa ya aina yoyote ile,jambo hilo likamchanganya akili yake kupita kiasi.
“Nani kaifunga akaunti hii tena?”
Mama Marietha ilibidi amuulize ‘Branch Manager’ aliyeitwa Kanei Mhando baada ya kuingia ofisini kwake,alitaka kujuwa mchakato mzima jinsi mambo yalivyokwenda.
“Subiri kidogo!”
Mwanamama mtu mzima mweupe aliyevaa miwani ya macho,akasimama kidogo na kutoka ofisini ambapo alimuacha Mama Marietha.Alivyorudi na kuketi alikuwa ana makaratasi mkononi mwake,akaketi na kuanza kubonyeza kompyuta yake.Huko alikuwa anatafuta mmiliki halali wa akaunti hiyo yaani ‘bank holder’ na sababu ya kufungwa kwa akaunti.
“Aliyefunga akaunti hii anaitwa Deo Karekezi,nadhani ndiye bank holder alikufungulia akaunti yako Mlimani city kwahiyo ukitaka kujua chanzo unaweza ukaenda Mlimani city”
Kanei Mhando alimaliza na kumuangalia Mama Marietha ambaye aliyeonekana kuchoka baada ya kupokea majibu hayo,alihisi kuishiwa nguvu sababu hakuwa hata na senti tano mfukoni mwake.
“Lakini huwezi kuniambia kwanini aliifunga?”
Mama Marietha aliuliza swali ambalo alishajibiwa kwenye maelezo yote.
“Hapana labda uende Mlimani City,Ahsante”
Mama huyu meneja wa Benki alimaliza na kutupa macho yake juu ya kioo cha kompyuta na kuendelea kubonyeza ‘keyboard’
“Lakini mwanangu nina shida”
“Kama kuhusu akaunti ungeenda mlimani city Mama,kwa sasa hivi sina cha kukusaidia”
“Nina shida nyingine”
“Shida gani?”
“Sina hata shilingi moja hapa mfukoni na nimetoka mbali Mwanangu naomba unisaidie japo nauli”
Kanei Mhando alimuangalia Mama Marietha kwa kitambo kidogo,kuna jambo ilionekana alikuwa akitafakari huruma ikamuingia,akajisukuma kwa nyuma kiti kilichokuwa na matairi kikaserereka akachukuwa pochi yake na kufungua zipu ambapo alichomoa noti ya shilingi elfu kumi,Mama Marietha akakabidhiwa,hakuamini!
Kwake pesa hiyo ilikuwa kubwa sana kwa siku hiyo,shukrani alizotoa hazikuweza kuelezeka kiwepesi.
****
Marietha alibaki kinywa wazi Mama yake alivyorejea nyumbani na kumueleza kila kitu,hakutaka kuamini kwamba Deo amefanya kitu kama hicho,alijaribu kutafakari vitu vingi na kushindwa kuelewa ni kitu gani kikubwa kibaya alichomfanyia Deo mpaka amfanyie mauzauza kama hayo,siyo hivyo tu.
Ndani hawakuwa na akiba ya pesa hata moja,hawakujuwa siku inayoitwa kesho wangekula nini.
“Mwanangu jikaze mimi mama yako wacha nipambane”
“Sawa Mama”
Siku hiyo usiku walilalia Ugali na Matembele,hiyo ilitokana na Mama Marietha kutumia chenji ya shilingi elfu kumi aliyopewa na meneja wa benki kama nauli.

Hali ilizidi kuwa mbaya sana nyumbani kadri siku zilivyozidi kuyoyoma, hapo ndipo Marietha alianza kuwakumbuka marafiki zake ambao alikuwa anakula nao bata kipindi yupo na Deo.Alivyowatafuta wote walimtosa na kumtolea nje,hakuna siku aliyohisi uchungu kama siku hiyo alivyofukuzwa nyumbani kwa rafiki yake kipenzi aliyeitwa Sharifa Mohamed.
“Embu nenda Marietha…Kaombe msaada msikitini”
“Shar…”
“Nenda nje Marietha sina msaada wa kukupa”
Haikuwa rahisi kuamini kwamba marafiki zake waliokula pamoja leo hii wamempa kisogo,alitamani kitu kinachotokea kiwe ndoto ili ashtuke!Lakini ulikuwa ni ukweli halisi,dunia ilianza kumpa kisogo ikawa imebinuka juu chini,chini-juu.Alitegemea kwamba rafiki yake walau angempa pesa kidogo ya nauli ili imrudishe alipotoka lakini haikuwa hivyo,alianza safari ya kurudi kwa mguu na kutoka Tabata Majumba sita mpaka alipokuwa anaishi kwa Mama yake haikuwa kazi rahisi kutembea kwa miguu,kulikuwa kuna kipande kirefu licha ya yote alikuwa ana ujauzito mkubwa sana.
Jua lilikuwa kali la saa saba na lilikuwa halali yake sababu lilimchoma utosini lakini alipiga moyo konde na kuzidi kusonga mbele kwa tabu,alihisi miguu yake inawaka moto kwa kuwa alitembea kwa umbali wa kama kilomita tano,alivyofika kituo kinachoitwa kwa Bibi aliona mti mkubwa akapumzika ili baada ya dakika kadhaa asimame na kuendelea na safari.
Zilipita kama dakika kumi na tisa nzima akiwa chini ya mti wa mbuyu,ghafla gari aina ya Landcruise Vx ikasimama kandokando ya miguu yake,hakuweza kuona watu waliokuwa ndani sababu ya vioo kuwa vyeusi.
Kioo taratibu kikaanza kushuka sura aliyoiona ilimshtua,moyo wake ukapiga kwa nguvu.
“Marietha”
Alikuwa ni Deo yupo nyuma ya usukani akiita kwa sauti ya chini kabisa akiwa haamini mtu anayemuona na alikuwa akimuangalia Marietha kwa macho yaliyojaa huruma ya waziwazi na macho yake yalilengwa na machozi.Alitamani kushuka lakini pembeni yake alikuwa ameketi Leila.
“Deo kwanini umepaki gari,unataka kununua nini?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Leila,hakuelewa kwanini gari limesimamishwa eneo hilo.
“Deo naongea nawewe”
Leila akauliza tena na kuchungulia,hapo ndipo alipopandisha mori baada ya kumuona Marietha.
“Deo washa gari tuondoke kumbe umesimamisha gari kisa huyo kenge wako?”
“Leila,wacha nikamsaidie”
“Weee ishia hapohapo,apande yeye mimi nishuke.Chagua kimoja”
Leila akauliza na lilitakiwa litolewe jibu la papo kwa hapo,Deo alikuwa ameganda kama barafu anamtizama mkewe, kuna vitu vilikuwa vinampitia kichwani,akatamani kushuka ndani ya gari lakini akashindwa.
“Deo”
Leila akaita,Deo alivyogeuka akakumbana na sura ya Leila iliyokuwa imejikunja amekasirika kuliko kawaida,hapohapo akaweka gia na kuliondosha gari.Hakuna siku aliyoumia moyo kama siku hiyo, Deo alikuwa anaendesha gari huku akimkumbuka Marietha lakini hakuwa na jinsi.
***
Marietha alibaki akilia machozi tu,akajizoazoa na kuendelea na safari yake,ambapo mbele alipata msaada,akapandishwa ndani ya bajaji na wasamalia wema wenye roho nzuri sababu walimuonea sana huruma kisha safari ya kupelekwa anapoishi na mama yake kuanza.
Alikuwa hoi bin taaban,dakika arobaini baadaye alikuwa anakaribia kufika, kwa mbali alimuona Mama yake yupo nje ya geti,magodoro na mabegi yapo kando yake vilevile,akashindwa kuelewa ni kitu gani kimetokea.
“Kaka nishushe hapo nishafika”Alimwambia dereva.
Dereva wa bajaj alivyolikaribia geti jeusi akasimamisha, Marietha akashuka.
“Mama kuna nini?”
Ndilo lilikuwa swali la kwanza kuuliza Marietha!
“Deo kachukuwa nyumba yake”
Mama alisema kwa uchungu sana huku akimuangalia mwanaye!



Ulikuwa ni huzuni mkubwa,hakuna mtu yoyote ambaye angeaminika kwa kusema kwamba Deo Karekezi ndiyo anafanya vitu kama hivyo,ilikuwa ni kama filamu ya kihindi tena ya kuuzunisha sababu hawakuwa na pa kwenda,mambo yalibadilika ghafla yakawa kinyume.Mama Marietha alitia huruma,Marietha aliumia moyo, bado hakutaka kulipitisha swala hilo moja kwa moja katika akili yake kuwa Deo ndiyo anafanya unyama kama huo,kiapo walichokula kanisani kwamba wataishi wote kufa kuzikana sasa kiliyeyuka,ilikuwa ni ngumu kumeza!
“Mama,sasa tutafanya nini?”
Marietha aliuliza huku uso wake ukionesha kuchoka na machozi yakimlenga.
“Sijui mwanangu”
“Deo ndiyo alikuja hapa?”
“Hapana”
“Nani alikuja?”
“Kawatuma watu,nilivyompigia simu akapokea mwanamke aliyedai ni mkewe”
Marietha aliumia na kuhisi uchungu ajabu moyo ulimuuma sababu muda mfupi uliopita alipishana na Deo akiwa na Leila, kivyovyote vile mama yake aliongea na Leila hilo lilikuwa wazi kabisa,lakini Marietha alimezea.
“Mama nataka niende kwa Deo sasa hivi”
“Kufanya nini?”
“Narudi,nisubiri”
Marietha alianza kutembea kwa tabu sababu ya uzito wa tumbo lake lililokuwa na mimba.
“Marietha”
Mama akamuita mwana.
“Abee”
“Unaenda wapi?”
“Kwa Deo”
“Kufanya nini?”
“Mama wacha niende”
Swala hilo lilimshangaza sana Mama yake,kwa unyama aliowafanyia mwanaume huyo ulitosha kabisa kuona hafai kwa maana hiyo hakutaka kuona mwanaye anarudi tena,kumruhusu mwanaye kwenda kwa Deo kulimaanisha kumruhusu mwanaye aende Jehanam ndiyo maana akamshika mkono.
“Wewe Marietha,nisikilize mimi Mama yako”
“Mama naomba niende”
“Siwezi kukuruhusu,unaenda kufanya nini?”
“Kuchukuwa vitu vyangu”
Haikuwa kazi rahisi kumzuia Marietha kufanya kile alichokiamua.Nia yake ilikuwa ni kwenda kwa Deo na kuchukuwa kilicho chake kisha kuondoka zake ingawa hakujuwa ni wapi atakwenda baada ya hapo.Akatembea mpaka zilipokuwa pikipiki nyingi,akapunga mkono, dereva wa pikipiki akamwendea mpaka miguuni mwake.
“Kimara,stop over.Pale stendi tunaingia kwa ndani kidogo”
“Poa panda”
“Shilingi ngapi?”
“Buku sita”
“Sina pesa lakini nataka nikupe simu yangu,unanipeleka na kunirudisha kuna vitu ninaenda kuchukuwa”
Hakuwa hata na thumni mfukoni hapo alipo, ilibidi atoe simu yake mfukoni yenye thamani ya shilingi laki sita ili asafirishwe.
“Samsang hii?”
Dereva wa bodaboda akauliza na kuichukuwa simu aliyoshika Marietha ilikuwa ni simu kali tena ya kisasa!
“Ndio ni s4”
“Kwahiyo niichukuwe?”
“Kaa nayo nikipata pesa yako utanipa simu yangu”
“Poa panda sista”
Marietha akapanda nyuma ya pikipiki na kukaa kwa upande mmoja,safari ikaanza mara moja ya kwenda nyumbani kwa Deo ingawa hakuwa na uhakika kama angemkuta.
***
“Sasa milioni tatu ya nini?”
“Baby bwanaa”
“Juzi tu nilikupa laki tisa jana laki tano.Leo unataka milioni tatu?hizo pesa zote natoa wapi baby”
“Sijui lakini mimi nina shida”
“Hiyo shida huwezi kuniambia?”
“Baby, are you gona give me or not?”(Mpenzi utanipa au hunipi)
Ilikuwa ni sauti ya Leila akiwa chumbani na Deo,Mwanamke huyu alijuwa kuzitumbua pesa za Deo sio kawaida na alimkwangua ipasavyo,nyuma ya mambo hayo kulikuwa na nguvu za giza.
Deo hakuwa mwepesi kutoa pesa lakini kizizi kilifanya kazi yake,alilishwa limbwata na alichokuwa anataka Leila kutoka kwake basi kilitekelezwa,akashikwa mapembe mbaya zaidi alichoharibu ni kumtambulisha Leila ofisi zake zote,alichokuwa anafanya Leila ni kupita na kuchukuwa pesa,kila baada ya siku mbili kupita,hiyo ndiyo ikamchanganya Deo akili.
“No siwezi kukupa,unatumiaje pesa kiasi hicho?Hivi unajuwa ni kasi gani umetumia ndani ya huu mwezi?Unajua kiasi gani?”
“Baby lakini si nina shida nimekwambia,sijataka unieleze”
“Shida gani hizo zisizoisha?hata mimi nina shida zangu vilevile.Haya unataka nyumba ile ya Mama Marietha niuze alafu iweje?”
“Mambo ya nyumba sasa yameingiliana vipi,ile nyumba niachie mimi nitajua cha kufanya wewe ushawafukuza inatosha,baby nisaidie na hizo pesa basi”
“Hiyo pesa sina,labda nikupe nusu yake”
“Basi sina shida,baki na pesa zako.Siku hizi si unajifanya umeota mapembe”Leila akajifanya kususa ili kupima maji!
Deo hakuwa mwanaume mwenye amani ndani ya nyumba yake tangu Marietha aondoke hilo alilijuwa lakini hakuwa na jinsi ya kufanya alijihisi kumpenda Leila lakini kuna kitu kilikuwa kina utofauti mkubwa sana nayo ni amani.
Kila kukicha Deo na Leila walikuwa wakikwaruzana.
“Basi nakupa milioni moja,nyingine utampigia Agness akupe”
“Woow thank you!”Leila aliruka ruka mikono yake ikiwa juu hewani,kwake ilikuwa kama bingo kupata mkwanja huo mrefu ili aende kutanua na marafiki zake ingawa mimba yake ilikuwa imetoka hilo alikumuumiza kichwa,alichowaza yeye ni kutanua tu na kuzitumbua mali za Deo.
“Alafu baby ulishaongea na polisi kuhusu ile kesi?”
“Ndio,nishamalizana nao,ondoa shaka”
Kesi iliyokuwa inawakabili yeye na Deo ni kumpiga na kumchangia Marietha lakini pesa iliongea, polisi wakazibwa midomo yao,wakaacha kuchonga!
“Okay baby ahsante,mimi ndiyo maana nakupenda”
“Sawa naomba nipumzike kidogo,kichwa kinaniuma”
“Okay mimi ninatoka”
“Fine”
Deo alikuwa kitandani amelala,akajigeuza upande wa pili ili autafute usingizi.
“Kwahiyo Agness anipe shilingi ngapi?”
“Chukuwa Milioni moja hapo kwenye dro,iliyobaki mwambie Agness akupe”
“Dro ipi?”
“Hiyo ya chini ya katikati”
“Sawa,alafu baby?”
“Sema”
“Unanipenda?”
“Ndio”
“Sasa mbona ulitaka kusimamisha gari ulivyomuona yule kenge wako?”
“Tafadhali naomba nilale.Kichwa kinaniuma”
“No nijibu”
“Nikiamka nitakujibu Leila,please nakuomba kwa sasa hivi nipumzike siko sawa.Naomba usinikere”Deo alijibu,ilikuwa kama kero tayari sababu Leila alimgasi mbali na hapo alihisi kichwa chake kinamuuma ndiyo maana alihitaji kupumzika!
Kwa furaha aliyokuwa nayo Leila, akatembea mpaka kabatini akachuchumaa na kuvuta ‘draw’ noti alizoziona zilimfanya atumbue macho,tangu amfahamu Deo hakujuwa kwamba kulikuwa kuna pesa nyingi kiasi hicho chumbani,udenda ukamtoka alikuwa ni kama fisi aliyeona mfupa!
Pesa zilikuwa zimepangwa, katikati kulikuwa na dola mia mia za kimarekani na yaliyobaki yalikuwa maburungutu ya shilingi elfu kumi za kitanzania.Alichofanya ni kuanza kuhesabu idadi ya pesa aliyoambiwa achukuwe,alivyohakikisha zimetimia shilingi milioni moja,akachukuwa simu yake na kumtafuta Agness Julius hewani,huyu alikuwa ni mmoja wa wafanyakazi wa Deo katika maduka yake ya ujenzi,ilivyopokelewa tu akaanza kusema anachohitaji lakini mambo yalikuwa tofauti.
“Hapana siwezi kukutumia mpaka nipate ruksa”
“Wewe Agness,embu nitumie hiyo pesa”
“Hapana siwezi kufanya hivyo nimesema”
Agnes Julius akakataa katakata,hakutaka kutoa pesa dukani bila ruksa kutoka kwa tajiri yake mbali na hapo alijuwa Leila ni awala tu hana mamlaka yoyote ya kutoa amri ndiyo maana akawa na kiburi.
Hiyo ilifanya Leila abenue mdomo na kusonya,akamsogelea Deo na kumtingisha kwa nguvu.
“Deo,wewe Deoo..Weweee”
“Leila,unataka nini lakini?”Akauliza kwa sauti iliyojaa hasira ndani yake sababu ndiyo alikuwa anachukuliwa na usingizi!
“Ongea na kahaba wako,hataki kutoa pesa mwambie anipe”
Simu ilitupwa kitandani hiyo ikamfanya Deo apapase na kuichukuwa,kilichofuata hapo ilikuwa ni sauti ya kufoka iliyoambatana na ukali juu yake,baada ya dakika mbili ujumbe wa meseji ukaingia kwamba salio lilitumwa kwenye simu ya Leila,haraka akaingia bafuni na kujimwagia maji,alivyotoka alichukuwa kimini na kukiweka mwilini,akatupia na top,akachukuwa funguo za gari na kubeba simu yake.Kabla ya kutoka mlangoni akasikia ujumbe wa meseji umeingia kwenye simu yake.
‘MAMBO TS ME RASHID TENGEZA,U GAVE ME YOH NAMBA JUZI MLIMANI CITY,CAN WE MEET TODAY FOR SMALL TALK NA SOME DINNER,BLUE PEARL GARDEN?’
Leila aliusoma ujumbe wa meseji huku akinyonga kitasa cha mlango,akili yake ikarudi nyuma kwa kasi ya mwewe,akamuona kijana mtanashati mrefu futi nyingi kwenda hewani,mwenye mwili wa mazoezi siku hiyo alivyokuwa na Deo mlimani City,tena walikutana chooni hapo ndipo alipoombwa namba za simu na kutoa.
“Griii griiii”
Simu yake ikaanza kuita akiwa bado anatafakari na namba alizoziona ndizo zilikuwa zinamtumia meseji,akatafakari kwa muda na kuipokea simu,akaiweka sikioni!
“Hi,Watsap”
Sauti kutoka upande wa pili ikasikika tena kwa ung’eng’e ikimsabahi.
“Cool, who could this be?”(Poa,nani mwenzangu)
Leila nayeye akateleza kimombo, kwake ilikuwa ni kama amezaliwa nacho sababu aliishi sana Uingereza na aliongea kiingereza kilichonyooka kama mzungu ingawa alikuwa Muafrika.
“Rashid Tengeza,We met at Mlimani city juzi i think.You gave me your digits.how is going?”
“Fine,sorry im kind busy now,I’ll get back to you later”Akakata simu.
Leila akajifanya ana kazi za kufanya na kumuhaidi Rashid Tengeza kwamba angempigia baadaye,alivyofungua mlango wa seblen ili kutoa nje.
Akabaki ameganda,ilikuwa ni kama kaona ajali sababu macho yake yalituwa kwa Marietha akiwa getini anaingia ndani,hasira zilimkaba kohoni hasa alivyoona tumbo la Marietha lilivyokuwa kubwa.
“Umesahau nini?”
Leila akauliza kwa hasira!


Marietha alifika nyumbani kwa Deo akiwa hoi bin taaban,isingewezekana hata kidogo kwa mlinzi wa getini kumfungulia geti lakini siku hiyo ilikuwa kinyume chake kwani geti lilifunguliwa.
“Mama karibu sana”
Marietha alikaribishwa kwa tabasamu na Mlinzi huyu,kitendo cha kuingiza kanyagio lake ndani macho yake yakakumbana na Leila anafungua mlango.Hakuwepo hapo kwa ajili ya shali kilichomleta ni vitu vyake kisha aondoke zake.
“Umesahau nini?”
Ingawa alilisikia swali lakini hakutaka kujibu kitu chochote kile akabaki anamtizama Leila aliyekuwa mbele yake anapiga hatua chache akimsogelea.
“Nimekuja kufuata vitu vyangu”
Hatimaye akajibu.
“Wewe una vitu hapa?Vitu gani?”
“Deo yupo?”
“Wanaume za watu unawaulizia wanini sasa hivi?”
“Nimekuja kufuata vitu vyangu ili niwaache na amani”
“Unachekesha kweli,embu nitokee hapa.Una vitu gani wewe?Nawewe aliyekutuma ufungue geti nani?Nani kakupa ruksa ya kumruhusu huyu golila aingie”Leila alifoka kwa sauti.
Sio kwamba Biko hakutaka kujibu swali hilo,alikuwa ana majibu mengi ya chooni lakini hakutaka kuruhusu kinywa chake kufanya hivyo kwani kibarua chake kingeota nyasi mara moja endapo Deo angesikia, sababu alielewa ni jinsi gani tajiri yake anavyompenda mwanamke huyu Leila,kumtukana ilimaanisha ilikuwa ndio tiketi yake ya kuondoka,akameza fundo la mate bila kujibu lolote.
“Nakuuliza wewe,Umechoka kazi?”
“Hapana Mama nisamehe”
“Nimwambie bosi wako?”
“Hapana”
“Aya mtoe upesi”
Hiko kilikuwa kibarua kingine kizito kwake sababu alimuonea huruma sana Marietha mbali na hapo alikuwa ni mjamzito.
“Biko,hunisikiii.Itoe hii takataka nje kabla sijaita polisi”
Marietha alikuwa katikati anafukuzwa kutoka nje tena kwenye nyumba ya mume wake wa ndoa jambo ambalo hakutaka kuliamini,akamgeukia Biko na kumtizama kwa macho yaliyojaa huruma nyingi.
“Usijali Biko mimi ninaenda”
Marietha akasema kwa masikitiko makubwa sana,alikuwa mpole.
“Pole sana”Biko akasema.
“Ahsante”
Midomo ya Marietha ilikuwa imemkauka,hakuingiza kitu mdomoni kwa takribani siku mbili.Alikuwa ana njaa kuliko kawaida lakini alijikaza,akatembea hatua chache na kulifikia geti kisha kugeuka na kuangalia nyumba kubwa ya Deo ambayo ilimkumbusha vitu vingi sana vilivyopita,alikumbuka maisha ya nyuma ya raha mustarehe yaliyopita.
“Biko”
Akaita kwa sauti ya chini.
“Naaam Mama”
“Una pesa yoyote unisaidie,maana sijala kaka angu tangu juzi nina njaa”
Marietha aliongea huku machozi yakimlenga,alitia huruma.
Biko akaingiza mkono mfukoni na alihisi mkono wake umeshika noti,akaitoa.Ilikuwa ni shilingi elfu mbili akamkabidhi Marietha.
“Nisubiri hapo”
Biko akaingia ndani ya kijumba chake na kutoka na ‘Hotpot’ ndani lilikuwa na chakula chake,ilikuwa ni bora yeye ashinde na njaa lakini atoe msaada huo,akamkabidhi Marietha.
“Wewe Bikooo”Leila akaita na kuanza kutembea kuelekea getini.
Kitendo cha mlinzi kuchukuwa ‘hotpot’ na kumkabidhi Marietha kilimkera sana Leila,akasogea mpaka karibu yake,akampokonya Marietha ‘Hotpot’ na kulifungua akamwaga chakula chote chini,zilikuwa ni ndizi na nyama.Njaa aliyokuwa nayo Marietha ilitisha alitamani ainame chini na kuokota ndizi moja moja ale,akabaki kukiangalia chakula kilichokuwa chini.
“Toka nje wewe mwanamke usinitafutie kesi hapa.Nawewe Biko kuanzia leo sahau kula chakula hapa ndani,Shenzi wewe”
Marietha alisukumizwa nje na Leila,bahati mbaya akajikwaa na chuma cha geti kilichokuwa chini akadondokea tumbo.
Leila hakujali akafunga geti,ambapo alitembea mpaka kwenye Landcruiser Vx na kufungua mlango.
“Pii piiiiii”
Akapiga honi hata kabla hajawasha gari kumaanisha kuwa geti lifunguliwe,mlinzi wa getini akafanya kazi yake.Akasukuma geti,Leila akazungusha funguo akakanyaga breki na kushika gia ambapo alibonyeza na kurudisha mpaka kwenye herufi ‘R’ gari likaanza kurudi kinyume nyume,akakunja kona kidogo na kukanyaga breki,akarudisha gia herufi D na kuzungusha tena usukani tayari kwa kutoka nje ya geti,akiwa ndani ya gari alimuona Marietha amelala nje,analia.
“Piii piiiii”
Honi hiyo ilikuwa kwa ajili ya Marietha atoke, ili atoe gari.Akashusha kioo.
“Wewe Bikoo,umtoe huyo Malaya hapo getini maana nitamkanyaga nimuuwe”
Mlinzi wa getini akatoka nje,akamuinua Marietha aliyekuwa analalamika kwamba tumbo linamuuma,akamuweka kando kitako.
Leila akatoa gari taratibu alivyokunja kona akasimama,gari lilikuwa limempa mgongo Marietha na alikuwa ana wasiwasi kwani endapo lingerudi nyuma basi lingemkandamiza kwenye ukuta na kumuuwa hapohapo hicho ndicho kitu alichokuwa anawaza Marietha,kifo cha kugongwa na gari sababu aliijuwa roho ya Leila.Gari lilisimama kwa kama sekunde moja mbele bila kuondoka.

Ni kweli Leila alikuwa ndani ya gari anamtizama Marietha kupitia kioo cha ndani katikati,akili yake ilimwambia arudi nyuma kwa kasi amgonge,akatafakari kidogo.Na kurudisha gia mpaka herufi ‘N’ yaani neutral,hapohapo akakanyaga mafuta mengi,moshi mwingi ukatoka kwenye ‘exsoce’akakanyaga tena mpaka mwisho.Moshi mchafu wa gari ulikuwa ukiingia puani kwa Marietha akawa ana kohoa sababu alikuwa akipaliwa,ulikuwa ni moshi mbaya sana wenye sumu kali.
Leila alifanya hivyo kwa sekunde kumi nzima.
“Si una njaa,kula moshi huo”
Akajisemea,alivyoridhika akaweka gia na kulitoa gari kwa kasi.
Akatokomea kwenye moja ya kona,akavuta mkanda wa gari na kufunga,hakujali kilichojiri huko nyuma alichowaza yeye kwa wakati huo ni kwenda kutanua na marafiki zake.Akapapasa mkono wake mfukoni na kutoa simu yake,akaingia kwenye Phonebook,mkono mmoja ukiwa juu ya usukani.
Akawa anatafuta majina mpaka alipolifikia jina HALIMA KUSSI,akaipa simu okay na kuiweka sikioni.Wakati huo macho yake yalikuwa huku na kule akitizama magari,alivyoona yameisha akaingiza gari barabara ya lami.
“Wee Halima,uko wapi?”
Alianza kuuliza baada ya simu kupokelewa.
“Leila muda wote tunakusubiri best,Where are you then?”
“Ndio natoka home,where are we suppose to meet?”
“Njoo Kibo complex,uwahi sasa”
“Ndiyo wapi hapo?”
“Sorry,Tegeta huku.Ukifika Tegeta mwisho nipigie”
Akakata simu na kuingia upande wa pili yaani ‘High way’akakanyaga mafuta mengi gari likasonga mbele kwa kasi,mfukoni alikuwa ana salio la kutosha ndiyo maana alikuwa mwenye furaha moyoni,siku hiyo alipanga afunge mwaka,na alitaka kuunguza shilingi milioni mbili na ndiyo maana aliwatafuta marafiki zake wa siku nyingi kabla ya kwenda Uingereza,dakika arobaini baadaye alikuwa Tegeta mwisho,akaweka gari kando na kusimama,hapo hakuelewa aende wapi akamtafuta Halima Kusi ili ampe maelekezo.
Haikuwa kazi ngumu kunasa maelekezo.Akawasha gari,akatizama ‘Site mirror’ili kuangalia usalama wa magari yanayopita na barabara ilivyokuwa nyeupe akangia,dakika kumi zilikuwa nyingi,akawa nje ya jengo kubwa lililoandikwa KIBO COMPLEX hapohapo akaegesha gari na kumpigia Halima Kussi,wakaonana.
“Shooogaaaa,Leiiila.Oh My God,is that you?”
Halima Kussi alikuwa ni msichana mdogo mrefu na mrembo,ungemuangalia harakaharaka ungemfananisha na mnyama twiga,alikuwa ana mikogo ya kisista duu.Walivyoonana walikumbatiana kwa furaha na kupigana mabusu ya mashavuni.
“Halima,Real?Look at you”
Leila nayeye akachombeza,ilimradi furaha sababu hiyo ilikuwa mara yao ya kwanza kukutana tangu arudi kutokea nchini Uingereza.
“So Watsap,how is U.k?”
“Hakuna chochote ushenzi tu”
“Don’t tell me now una drive”
Halima alivyoona gari kubwa ya gharama ilibidi ahoji.
“Ni stori ndefu,lakini nimepata kibopa.Wabongo wanasema ana Mpunga,ana cash.Sio mbabaishaji”
Leila akajigamba.
“Sawa twende,Wakina Adela wapo ndani.Wanakusubiri”
Hapohapo wakaanza kuongozana ambapo waliingia ndani,kibo complex.
Furaha ikazidi kuongezeka maradufu.Kwa mbwembwe akamuita Muhudumu na kuagiza pombe kali.
“Wewe unakunywa nini?”Leila akamuuliza mmoja wa marafiki zake.
“Nakunywa Savvana”
“Mletee Savana tano,mimi niletee Dompo”
Ndani ya dakika moja meza ilikuwa na msitu wa chupa,kazi yao ilikuwa ni kunywa na kugongesha mikono na stori ziliendelea kama kawaida.
Kilichomuinua Leila ni simu,akatoka pembeni ili kuipokea.
“Halloo Leila,it’s me again, Rashid Tengeza”
“Okay nambie”
“Wewe ndiyo uniambie,give me plan”
“Sasa hivi nipo mbali kidogo na mabest zangu,kwanini tu si meet kesho”
“Where are you by the way?”(Uko wapi kwani)
“Hapa wanapaita Oh My God…jina limenitoka wanapaitaaa..Come on come on..Kibo yes Kibo Kibo Complex”
“That is good,kwa sababu nipo near by,mimi nipo hapa Salasala.So, can we link up?”
“Yeah sure,njoo lakini nitakuboa coz nipo na marafiki zangu”
“Ah no usijali kuhusu hilo,I’ll be fine”
“Okay,no Problem”
Leila akakata simu,akarudi kwa marafiki zake wakaendelea na stori na pombe zikaongezwa.
Muda ulikwenda mbio mpaka inafikaa saa mbili walikuwa tayari wamelipuka!
“Jamani sorry,kuna mgeni wangu anakuja hapa naona anapiga nadhani kashafika,ngoja nikamchukuwe hapo nje”
Leila aliwaambia marafiki zake sababu aliona simu kutoka kwa Rashid, akaipokea na kuanza kutembea kutoka nje.
“Yes hallo,ushafika?Nashuka hapa mlangoni njoo.Okay sawa”
Ni kweli walionana,Leila akabakia ameduwaa mwili wa mwanaumue huyu ulimfanya ashangae lakini sio sana.Rashid alikuwa mwenye kifua kilichotanuka na siku hiyo alivaa tshirt iliyombana mkono wake mkubwa ukajichora vizuri,kifua ndiyo usiseme.Na alikuwa mrefu kiasi.Kichwani hakuwa na nywele hata moja yaani kipara lakini mashavu na kidevu chake vilijaa ndevu nyingi.
Staili hiyo ya kunyoa ndiyo ilimfanya awe maridadi zaidi.
“Yoh Leila”
Walivyoonana wakaleta uzungu,wakakumbatiana na kuanza kuingia ndani,ambapo vinywaji viliongezwa,wakazidi kunywa pombe kali.
Katika hali ya kushangaza Leila alikasirika baada ya kumuona Halima Kussi anajitongozesha kwa mgeni aliyekuja naye,sababu alikuwa naye beneti.Mara ajipitishe mara washikane,hiyo ilimfanya apate wivu.Kilichomuuma zaidi ni baada ya kuona kitendo cha Halima kumkalia Rashid Mapajani.
“Wewe Halima,mbona unakuwa sioo mstaarabuuu”
Leila aliongea huku akiwa amekunja sura.
“Kwani vipi?”
“Vipi hujui,hujui au?Wewe unamjua huyo?”
“Ndio tumejuana hapa”
Kitendo hicho kilimfanyua Leila asimame wima, kwa hasira akamvuta Halima pembeni na kumshika Rashid mkono.
“Lets goo”(tuondoke)
Leila akatoa kauli hiyo,akamvuta Rashid mpaka nje kwenye maegesho ya magari.Wakaingia ndani ya gari.
“Tuondoke hapa siooo pazurii,hawa marafiki zangu usizoeane nao.Makahaba”
Kwa akili ya ki utu uzima na ujanja wa mjini Rashid Tengeza alielewa nini maana ya mwanamke huyo kufanya hivyo,hakutaka kulaza damu.
Hapohapo akamvaa Leila midomoni akaanza kumlamba midomo,ilikuwa ni kama mwanamke huyu alikuwa akisubiri kitendo hiko kwani nayeye alifungua mdomo wake wakaanza kulana denda kwa fujo!



Deo Karekezi alizinduka kitandani saa tatu ya usiku,baada ya kulala masaa mengi tangu jioni ya siku hiyo kutokana na uchovu,usingizi ulikuwa mwingi kichwani.Ndani kulikuwa kuna giza totoro sababu taa zilikuwa hazijawashwa,akapapasa mkono akijaribu kama atagusana na Leila lakini haikuwa hivyo,mkono wake uliendelea kupapasa kitanda bila kuambulia kitu chochote.Akarudisha mkono kwenye kitanda ambapo kulikuwa na soketi ya kuwashia taa ndogo,akabonyeza mwanga ukatokeza.
Akatizama huku na kule ili kumuangalia Leila lakini hakuwepo.
“Leila!”Akaita huku akitizama mlango wa bafuni akidhani wenda atakuwa anajimwagia maji,lakini hakuitikiwa.Akajiinua kiuvivu na kutembea mpaka bafuni ambapo huko alitoa haja ndogo na kurudi kitandani,akili yake bado haikukaa sawa,akatembea mpaka mlangoni akanyonga kitasa ili aende seblen ili akutane na Leila lakini Seble ilikuwa kimnya,hakukuwa na dalili ya Leila kuwepo.Akatoka mpaka nje kabisa.
“Bikooo”
“Naa! Naaam! Naaam! bosi”
Mlinzi wa getini akapata kiwewe,akaweka redio yake ya mbao chini na kutembea mpaka kwa tajiri yake mikono nyuma kwa adabu zote.
“Naam bosi”
“Huyu Leila yuko wapi?Alitoka leo?”
“Ndio Bosi”
“Saa ngapi?”
“Saaa saaa!”
Mlinzi akasita kidogo sababu hakuwa ana uhakika Leila aliondoka saa ngapi sababu hakuwa na saa ya mkononi.
“Jioni jioni hivi”
Deo alivyoangalia nyuma akaona gari aina ya Landcruiser vx halipo,hilo likawa jibu tosha kwamba Leila hayupo ndani ya nyumba akarudi ndani,akapitiliza mpaka chumbani ili kuchukuwa simu amtafute hewani lakini simu yake haikuwa na chaji,ilizima!
Akatafakari kidogo na kuichomeka kwenye soketi ya umeme.Akatoka na kuingia jikoni ili kuangalia kama kuna chakula,jikoni kulikuwa kweupe hakukuwa na mabaki yoyote yale.Hiyo ikamlazimu achukuwe macaroni apike ale,tumbo lake lilivyokaa sawa akajitupa juu ya sofa akawasha televisheni,hakukaa sana usingizi ukamzoa.

Alivyoyafumbua macho yake cha kwanza, aliyatupa juu ya saa kubwa ukutani ilikuwa tayari saa tano ya usiku,akasimama na kutembea mpaka kwenye dirisha akavuta pazia,gari yake bado ilikuwa haijarudi kumaanisha kwamba Leila bado hajarejea,akarudi chumbani haraka akachomoa simu,akaiwasha na kuanza kumtafuta Leila hewani ili kujuwa ni wapi alipo!
****
Midomo yao ilikuwa imegandana kama gundi,walikuwa wakilana denda ndani ya gari tena kwa fujo kana kwamba waliambiwa wanakufa Kesho,Sio Rashid wala Leila kila mtu alimnyonya mwenzake ulimi kwa pupa,mkono wa Rashid taratibu ukawa una kazi ya kupapasa kifua cha Leila,hakuishia hapo akabinua blauzi aliyokuwa ameivaa kwa juu, chuchu zikawa nje akaanza kuzibinya mithili ya mtu anayechagua maembe gengeni,kidole kimoja kilikuwa kinashika chuchu.Mwanaume huyu Tengeza hakuishia hapo,akateremsha mkono chini mpaka juu ya kitovu cha Leila kilichokuwa laini sana,hapo akaperuzi na kuzidi kudidimia chini,akapangua chupi,akapitisha kidole kimoja katikati ya mapango.Mgodi wa Leila ulikuwa umelowa vibaya sana,hiyo haikufanya Rashid asitishe zoezi lake alilolianza kwa kutumia kidole chake cha katikati akaingiza kwenye mgodi,hapo ndipo Leila alipoanza kukinyonga kiuno chake ilielekea kwamba alihisi raha za ajabu.
“Griii griiii,Griii griiiii”
Simu ya Leila ilianza kuita, alisikia hilo lakini alipuuza hakutaka kukatishwa raha zake hata kidogo ndiyo maana akaendelea kulana denda na Rashid,alivyoona kuna nafasi finyu akapitisha mkono wake mmoja chini ya kiti kikalala, hiyo ilimaanisha kwamba mchezo kaufagilia.
Mwenyewe kwa hiyari yake akaanza kutoa nguo zake,Rashid nayeye hakupoteza wakati,kufumba na kufumbua wakabaki kama walivyozaliwa.Mguu mmoja wa Leila ukawekwa begani,Rashid akachukuwa mkia wake na kuutumbukiza shimoni.
“Aaaaah”
Huo ndiyo mguno wa chini alioutoa Leila baada ya mkia kuingia ndani ya shimo lake.

***
“Piii piiii piiiiiiii”
Ilikuwa ni saa tisa ya usiku Leila alikuwa akipiga honi ili aingize gari ndani ya nyumba,ni baada ya kutoka kufanya ngono na mwanaume aliyeitwa Rashid Tengeza,alilifurahia tendo hilo na walihaidiana kwamba wakipata nafasi wakutane sehemu nzuri iliyotulia ikiwezekana wakodi hoteli,kifupi Leila alipagawishwa sio mchezo.
Kila wakati alikuwa akiwaza jinsi alivyokuwa amekunjwa anafanya mapenzi na mwanaume huyo ndani ya gari akaenda mizunguko mitatu kwa mpigo jambo ambalo hakuwahi hata kuota kufanyiwa,ni sawa Deo aliweza kufanya ngono lakini Rashid alikuwa kiboko ya yote!
“Pii piiii”
Akapiga tena honi,akiwa anasubiri geti lifunguliwe, zilivyopita dakika mbili geti likaanza kusukumizwa na mlinzi.Leila akaingiza gari ndani,akazima taa na kuzima gari pia.Akashuka,akatembea na kunyonga kitasa cha mlango taratibu, akavua viatu na kuanza kunyata,taa zilikuwa zimezimwa.Akaurudishia mlango kwa tahadhari,akaendelea kutembea taratibu bila kutoa kishindo, akaufikia mlango wa chumbani na kunyonga kitasa taratibu akaingia ndani na kufunga mlango,kwa mtindo huo huo akasogea,kabla ya kufika kitandani taa ikawashwa,moyo wake ukapiga paa, akadondosha mpaka pochi!
“Umetoka wapi?”
Swali hilo lilitoka kwa Deo akiwa ameketi juu ya sofa sura ilikuwa imekunjamana,macho mekundu amejawa na hasira kupita kiasi.
“Umetoka wapi?”
Akauliza tena,macho yake akiwa amemkazia Leila yupo mbele yake anatetemeka.
“Kwa kwa rafiki yangu”
Kwa mara ya kwanza Leila kutetemeka na kupata kiwewe macho makali ya Deo yalimtisha,hakuwahi kumuona Deo katika sura hiyo tangu amjuwe,ndiyo maana alihaha!
“Unajuwa sasa hivi ni saa ngapi?”
“Ndiyo,ni usiku sana”
“Nimekupa pesa zangu umeenda kulewa?”
Kilichofanya Deo aseme maneno hayo ni kwasababu ya harufu ya pombe iliyokuwa imeenea chumba kizima.
“Nilikunywa tu kidogo baby na is..”
“Shut up!”
Akamkatisha kwa hasira na kupaza sauti, akasimama wima,akasogea mpaka karibu na Leila.
“Lakini ba…”
“I said shut up!nimekuuliza ulikuwa unataka pesa zangu ili ukanywe pombe?hivi unadhani mimi sina shida na pesa,unajuwa nina zipata vipi?Nakuuliza wewe Leila,unajua hizo pesa unazochezea ninazipata vipi?”
Halikuwa tena swala la Leila kuchelewa kurudi bali kilichomuuma ni pesa zake nyingi alizotoa ambazo zilienda kutumiwa vibaya,hilo alilijuwa wazi sababu alimjuwa Leila ni mwanamke anayependa starehe mno!
“Hapana sio hivyo Love”
“Kumbe nini?Kumbe nini?Kumbe nini?”
Ndani ya chumba ukawa mzozo mkubwa ilikuwa kidogo makofi yatembee lakini Deo akajiepusha na hilo alivyokumbuka jinsi alivyompiga Marietha na kufunguliwa kesi.
Akanywea na kurudi kitandani,mikono yake ikiwa kichwani uso wake unaangalia chini,Leila alibaki amesimama kama mlingoti hajuwi ni kitu gani akifanye!
“Baby I’m sorry”(Mpenzi samahani)
Leila aliomba radhi kwa Deo lakini moyoni haikuwa hivyo,yeye alikuwa akifanya gelesha na alikuwa kama anaigiza kwani mawazo yake yalikuwa kwa Rashid Tengeza!
“Panda kitandani ulale”
Badala ya Leila kupanda kitandani akanyoosha mpaka mlango wa bafuni huko akavua nguo zake zote na kufungua bomba la mvua,maji yakaanza kumiminika .Sura ya mwanaume Rashid ikaanza kumpitia kichwani akawa kama anajiona jinsi alivyokuwa ndani ya gari ananyonga kiuno chake na kutoa miguno,akawa kama anaangalia sinema ya ngono,akatamani wakati huo awepo na mwanaume huyo kitandani.
“Kesho lazima nimtafute”
Leila akajisemea kimoyomoyo,akajisugua vizuri akachukuwa taulo akajipangusa na kurudi chumbani ambapo alimkuta Deo bado yupo macho,ilionekana bado alikuwa mbali kifikra!
***
“Mama Rebeca,sio Marietha yule?”
“Hapana sidhani”
“Ndiye yeye,sikutanii”
“Mh!Embu simamisha gari”
“Subiri nipaki hapo mbele hapa pabaya”
Zilikuwa ni sauti kutokea ndani ya gari aina ya Verossa,Mzee mwenye mvi chache kichwani mnene mwenye kitambi,alikuwa nyuma ya usukani anaendesha gari maeneo ya kinondoni kwa Manyanya,pembeni kushoto kulikuwa na mwanamke mnene mtu mzima.Kuna mtu walimuona na walimjua vizuri,ndiyo maana mzee huyu akaweka gari kando alivyopata upenyo,akachomoa mkanda kwa gari na kutanguliza kiatu chake aina ya mkuki moyoni.
Ilielekea alikuwa mzee mwenye heshima zake sababu ya muonekano tu.Akaangalia magari huku na kule, alivyohakikisha kuna usalama akavuka upande wa pili.
“Marietha”Akaita.
Maskini ya Mungu alikuwa amechakaa mno,ni kweli alikuwa Marietha tena mjamzito tumbo lilikuwa kubwa sana,amekaa chini ameweka kiboxi anaomba msaada kwa watu wanaopita njia na alivyoinua shingo yake juu alijisikia uchungu ajabu!
“Marietha”
Mzee akaita tena,akawa kama haamini mwanamke anayemuona,haikuwezekana hata kidogo kwa mwanamke kama huyo kuwa mahali hapo sababu mumewe alikuwa mfanyabiashara mwenye utajiri mkubwa.
“Shikamoo”
“Marahaba?Vipi?Kulikoni?.Embu simama”
Mzee huyu alitambulika kwa jina la Benjamin Ngowi,nayeye alikuwa ni mfanyabiashara mkubwa na alikuwa akitoa bidhaa kutoka nchini China kuleta Tanzania alikuwa ni mchaga wa Marangu,katika watu ambao walimfundisha Deo Karekezi biashara basi mzee huyu wa kichaga aliyekuwa na kiwanda chake cha viatu huko Mbagala alichokiita NGOWI LEATHER PRODUCTS hapo ndipo alipoupatia utajiri wake.
Badala ya Marietha kusimama yeye alianza kulia machozi.
“Simama Marietha,usilie”
Mzee Benjamin Ngowi,akainama kidogo na kumshika Marietha mkono.Wakatembea taratibu na kuvuka upande wa pili mpaka ilipokuwa Verosa yake inaunguruma akafunguwa mlango wa nyuma,akamuingiza Marietha ndani akazunguka upande mwingine, akaingia upande wa dereva.
“Marietha”
Mke wa Benjamin Ngowi aliyeitwa Haika ama Mama Rebeca akageuka na kumuita.
“Marietha”
“A..be aaaabee”
Hatimaye akaitikia huku kwikwi ikiwa imemkaba kohoni,alikuwa mchafu na nywele zake zilikuwa na vumbi zipo timtim.
“Baba Rebeca embu turudi nyumbani”
Haika,akashauri!
“Ndiyo nilikuwa nataka kufanya hivyo ngoja nigeuze gari,alafu naomba namba za Deo”
Mzee Benjamin Ngowi akaweka gia na kugeuza gari akarudi alipotoka,hawakuwa mbali sana na wanapoishi sababu waliishi Kinondoni hiyohiyo lakini kituo kinachoitwa Studio.
Dakika kumi baadaye walifika,wakaegesha gari nje ya nyumba yao wakazunguka na kumchukua Marietha wakaingia naye mpaka ndani.
“Weweee Sakinaaa,Sakinaaaa”
“Abeee Mamaaa”
Sakina alikuwa ni mfanyakazi wa ndani,alikuwa ni binti mdogo wa makamo,akatokeza mpaka seblen.
“Chemsha maji ya kuoga kisha weka bafuni”
“Sawa Mama”
Alivyotaka kuingia jikoni akaitwa tena.
“Chai iliisha?”
“Ndio”
“Tengeneza alafu nenda pale kwa Mangi kanunuwe mkate na siagi”
“Aya Mama”
Alivyotaka kugeuka akasimamishwa.
“Wewe Sakinaaa”
“Abeee”
“Zile nguo zangu kwenye beseni ulianika?”
“Hapana Mama”
“Sasa kwanini?Nenda kazianike”
Sakina alikuwa njiapanda,hakuelewa aanze kufanya lipi.Akili yake ikafanya kazi kwa kasi,akaingia jikoni akabandika maji kwenye gesi,akakimbia haraka mpaka uwani akatoa nguo ndani ya beseni akazianika na kutoka nje ya geti mpaka dukani kwa Mangi akanunua mkate pamoja na siagi na kurudi.

Marietha hakuwa na sababu ya kuficha kitu chochote kile,aliifahamu sana familia hiyo na aliiheshimu vilevile.Alimjua Mzee Ngowi na Mkewe,ki ukweli alihitaji msaada ndiyo maana akazungumza mambo yote,mpaka Deo akampiga mwisho akahitimisha kwamba Deo ana mwanamke mwingine tayari.Ilikuwa ni historia ya kuumiza moyo,Mama Rebecca akajikuta anadondosha chozi.Mzee Ngowi alijikaza kiume, alikuwa akisikitika huku akitingisha kichwa.
“Mama Rebecca naomba namba za Deo,Marietha ngoja niongee na Deo usijali kabisa.Alafu nenda mezani kanywe chai”
Namba zikatolewa hapohapo Mzee Ngowi akatoa simu yake kubwa,akaweka namba za Deo.
Akaipa simu 'okay' na kuiweka ‘loudspeaker’ alitaka kila mtu asikie.
“Griii griiiii”
Simu ilisikika ikiita,maana kwamba Deo alikuwa hewani ilikuwa asubuhi ya saa nne!
“Halloo,Mzee Ngowi shikamoo,za asubuhi? naona leo umenikumbuka mzee wangu”
Deo alikuwa hewani tayari,sauti yake ilienea sable nzima Marietha aliyekuwa meza ya chakula akasitisha kuweka kipande cha mkate mdomoni, nayeye akatega sikio.
“Kila siku nakukumbuka kijana wangu,niliibiwa simu.Ndiyo nimepewa namba zako hapa na Mama Rebeca,vipi lakini hujambo?”
“Sijambo mzee wangu,hofu kwako?”
“Mimi namshukuru Mungu,familia haijambo?”
“Haijambo kabisa”
“Mkeo Marietha mzima?”
Mzee Ngowi akazunguka kidogo!
“Yes mzima kabisa”
“Siku nyingi kweli,naomba nizungumze naye”
“Hapa hayupo,amesafiri.Mama yake anaumwa! sasa hivi yupo Tanga anamuuguza”
Mzee Ngowi akageuka na kumtizama Marietha,Deo hakujuwa kwamba mkewe anamsikia!



“Sasa Deo”
“Naam mzee”
“Naweza kuonana nawewe leo?”
“Saa ngapi?”
“Utatoka ofisini saa ngapi?”
“Saa kumi na moja hivi jioni”
“Saa moja naomba tuonane”
“Wapi?”
“Popote pale,kwangu kwako ama sehemu yoyote iliyotulia.Lakini ningependa uje kwangu”
“Sawa hakuna neno,nitakuja leo Kinondoni”
“Aya,kazi njema”
“Okay Mzee…tititiii”
Mazungumzo baina ya Deo na Mzee Ngowi yalihitimishwa hapohapo na kila kilichokuwa kinaongelewa kilisambaa seble nzima sababu ya simu kuwekwa ‘loudspeaker’.Moyo wa Marietha uliuma kupindukia,bado alikuwa amegandisha kipande cha mkate karibu na mdomo wake akawa ameganda kama barafu anamuangalia Mzee Ngowi.Mama Rebeca aliishiwa nguvu,akageuza shingo yake na kumtizama Marietha!
“Marietha”
“Abee”
“Kunywa chai,baada ya hapo uingie bafuni uoge uje tuzungumze”
“Ahsante”
Ilikuwa ni kama yupo kwenye mashindano ya kula vile,Marietha alifakamia mikate kama mchwa,alikula na kumaliza mkate mzima,hiyo ilitokana na njaa ya siku kadhaa bila kuweka kitu chochote mdomoni,baada ya hapo mfanyakazi wa ndani alimuonesha bafu la kuoga.
“Sakinaaaa”
Mama Rebeca aliita akiwa seblen.
“Abeee Mama”Sakina akatokeza seblen mikono nyuma anasikiliza maagizo ya bosi wake ama mama mwenye nyumba.
“Kuna nguo alizoacha Mama alivyokuja,mpatie Marietha akimaliza kuoga”
“Sawa Mama”
***
Maji aliyokuwa akijimwagia Marietha bafuni yalichanganyika na machozi lakini hayakuonekana sababu yalikuwa yanasombwa na maji,alilia kwa vitu vingi sana.Alihisi amebeba dunia nzima,mateso aliyokuwa anayapata yalizidi kipimo chake,wakati mwingine alianza kumtupia lawama Mungu kwa kumleta Duniani,hakuelewa ni kitu gani haswa alichofanya mpaka astahili adhabu kama hiyo.Marietha alikaa bafuni kwa takribani dakika thelathini ndipo akatoka akiwa amejifunika taulo,tumbo lipo mbele.Akakutana na Sakina katikati ya Kordo, akapelekwa mpaka chumbani ambapo huko alipewa nguo za kuvaa,akaziweka mwilini.Lilikuwa ni dera kubwa lenye rangi nyekundu,baada ya hapo akajiegesha kitandani,kabla ya kukaa sawa mlango wake ukafunguliwa,Mama Rebecca akaingia.
“Marietha,jisikie upo nyumbani.Hapa ni nyumbani kwako”
“Ahsante Mama”
“Pumzika,baadaye kidogo utaletewa chakula ili ule ama kama ukitaka kwenda seblen kuangalia angalia movie ni sawa tu,sisi tunatoka lakini tutarudi”
“Sawa Mama ahsante”
“Aya baki salama”
Mama Rebeca alizungumza kwa sauti yenye ukarimu wa hali ya juu,akiwa amesimama mlangoni,alivyomaliza anayotaka kusema akatoka na kufunga mlango huku nyuma akimuacha Marietha anaogelea katika kisiwa cha mawazo.
***
Akili ya Dokta Kapoor haikuwa sawasawa hata kidogo,aliwaza mamilioni ya pesa aliyohaidiwa endapo atakamilisha figo alizoambiwa azitafute,ilibaki figo moja ili idadi ya figo zinazotakiwa zikamilike kwa maana hiyo ilikuwa ni lazima afanye juu chini aipate.Baada ya kukaa sana chini,aliibuka na jambo lililomfurahisha kwamba achukuwe figo ya Issa,kijana ambaye anaishi nyumbani kwake.Usiku kucha hakulala alitamani kukuche mapema,kwake dakika moja ilikuwa kama mwaka siku hiyo.
“Vipi?”
Mkewe,Dokta Khaila ilibidi ahoji.Macho ya mume wake yalikuwa juu darini kayakodoa.
“Hakuna kitu,najaribu kutafakari mambo mawili matatu”
“Lala,leo umechelewa kurudi.Si unajuwa kesho kazini”
“Naelewa”
“Basi pumzika”
“Sawa”
Dokta Kapoor akageukia upande wa pili,lakini hakuyafumba macho yake bado aliendelea kupiga hesabu zake ni mbinu gani atumie sababu Issa alikuwa ni mzima wa afya,bora angekuwa kama kipindi cha nyuma mgonjwa mahututi wenda ingekuwa rahisi kwake.
“Hapa inabidi nitumie taaluma yangu vizuri,nishapata jibu”
Dokta Kapoor aliwaza akatabasamu ilionekana alipata wazo kabambe,akafumba macho yake usingizi ukamsomba.
***
Alikuwa wa mwisho kulala lakini wa kwanza kuamka,kitu kilichomuamsha siku hiyo ni Issa,alitaka kwenda chumbani kwake amchukuwe kisha waondoke wote na mbele ya safari huko amchome sindano za dawa kali,amchane tumbo achukuwe figo,hayo ndiyo mambo aliyokuwa anawaza usiku uliopita.
Akafika mpaka chumba anacholala Issa,akagonga mlango lakini hakuitikiwa,akagonga tena lakini wapi!akanyonga kitasa,mbele yake alikumbana na kitanda kitupu,Issa hakuwepo.
Akatoka nje na kuzunguka nyuma ya nyumba akimtafuta Issa kama yupo,sababu wakati mwingine alikuwa akifanya mazoezi lakini hakuambulia kitu,akarudi chumbani kwa mke wake.
“Khaila”
“Abee”
“Issa yuko wapi?”
“Chumbani kwake hayupo?”
Dokta Khaila akajibu kwa swali.
“Kama angekuwepo nisingekufuata na kukuuliza”
“Atakuwa na Katrina labda”
“Atakuwa na Katrinaa?Kivipi?”
“Jana aliniambia anataka kutembea kwenda kufanya shoping ya chuo hivyo ataenda na Issa asubuhi,wenda watakuwa wameenda”
“Tangu lini Katrina akafanya shoping peke yake?”
“Si yupo na Issa,hayupo peke yake”
“Nani kamruhusu?Mimi mbona sina taarifa?”
Dokta Kapoor alifoka mpaka mishipa ya shingo ikamsimama.Hakukasirika kwa kuwa Katrina alitoka bila kumuaga, nyuma ya hayo alikuwa ana mengine,alichukia sababu ya mamilioni yake ya pesa.Hakutaka kumsikiliza tena mkewe akatoka mpaka nje na kuwasha gari,akaondoka zake,akiwa amevimba kama chura!
***
Gari ndogo aina ya IST, ilikuwa nje kandokando kabisa ya bango lililoandikwa M&K guest house kwa juu na ilionekana aliyeegesha gari hilo nje ya nyumba ya wageni hakupenda ajulikane ndiyo maana akalificha ubavuni kabisa mwa ukuta,ni kweli haikuwa rahisi kwa mtu yoyote kuliona kiurahisi.
Chumba kilichoandikwa ‘Lion’ndicho Katrina na Issa walikuwepo ndani,wapo juu ya kitanda wanapigana mabusu ya midomoni wakinyonyana ndimi.Gia ya Katrina akitaka kwenda kununua vitu kwa ajili ya chuo ilizaa matunda na ndiyo maana siku hiyo wakawa ndani ya chumba wawili tu wanajivinjari,hakuna siku aliyofurahi kama hiyo ingawa mapigo yake ya moyo yalikuwa yakipiga kwa nguvu.Hakuwahi kufanya mapenzi na mwanaume yoyote yule tangu azaliwe ndiyo maana jasho lilimtoka na hakuwa ana uhakika kama atafanikiwa sababu alikuwa akisikia wenzake wakisema ni jinsi gani maumivu ya kutolewa bikra yanavyokuwa.Licha ya yote alipiga moyo konde ndiyo maana akatoa nguo yake ya juu akabaki na blazia, hiyo ilitosha kumaanisha kuwa picha limeanza,sio siri Katrina alikuwa ni mweupe mno sababu ya hasili yake.Waliendelea kunyonyana midomo yao taratibu mno,Issa alikuwa chini Katrina juu, akatoa sketi aliyokuwa nayo mwilini akabakiwa na chupi pamoja na blazia peke yake.Damu ya Issa ilikuwa inamwenda mbio kuliko kawaida,akahisi moyo wake umeacha kupiga kwa sekunde kadhaa.Msumari wake ulikuwa umesimama sawa sawia,nayeye akaona isiwe tabu akatoa suruali yake na kuvua shati harakaharaka,akapitisha mikono yake nyuma ya mgongo wa Katrina akafungua sidiria,hatimaye kifua cha binti huyu kikabaki wazi,akayafakamia maziwa na kuanza kuyanyonya.Raha alizokuwa anahisi Katrina hakuwahi kuzipata kabla,kwanza alihisi kama mwili wake mzima umepigwa ganzi ni baada ya kuhisi jotojoto juu ya chuchu zake,maziwa yake yalikuwa yakilambwa na ulimi wa Issa hiyo ilimfanya mpaka ayafumbe macho yake,akaingiza mikono yake mwenyewe ndani ya chupi yake akaanza kujisugua.Issa aliliona hilo,akachukuwa mkono wake taratibu na kuanza kuishusha chupi ya Katrina chini ingawa kwa mara ya kwanza haikuwa kazi rahisi.
“Isaa Nooo!”
Hivyo ndivyo Katrina alivyosema kwa sauti ya puani lakini hiyo ilikuwa kama staki nataka na mapozi tu ya kihindi ki ukweli mchezo huyo alitamani uendelee japokuwa alikuwa mwenye hofu.Issa hakutaka mchezo kabisa,akaitoa chupi yote,Katrina akabaki kama alivyozaliwa, alihisi kutetemeka mwili mzima,ilikuwa ndiyo mara yake ya kwanza kuvua nguo zake zote mbele ya mwanaume,alijisikia aibu.
“Aaah aaah ssshss”
Hakujijua kama anatoa sauti lakini alihisi vitu kama utitiri vinatembea ndani ya damu yake,akazidi kutoa miguno.Issa akajivuta akambinua yeye akawa juu yake,akaitanua miguu yake huku na kule.Akamuweka nyoka wake mrefu na mnene vizuri na kumsogeza shimoni.
“Issaaa noooooooo!”Katrina alipiga kelele,baada ya kichwa cha nyoka kuanza kuingia ndani ya shimo!
****
Deo Karekezi alizima gari akaretemka baada ya kufika nyumbani kwa Mzee Benjamin Ngowi usiku wa saa mbili,ilim-bidi awahi lakini foleni ya mjini ndiyo ilimfanya achelewe lakini hilo alilieleza kwa Mzee Ngowi hata kabla hajafika akiwa njiani,alivyofika getini akasimama ilionekana alisahau kitu ndani ya gari ndiyo maana akageuza,akafungua mlango wa gari na kuchukuwa simu zake mbili za mkononi,akafunga mlango tena.
Na kuanza kupiga hatua kuelekea getini,akagonga na kufunguliwa na msichana wa kazi.
“Habari Sakina”
Haikuwa mara yake ya kwanza kukanyaga nyumbani hapo ndiyo maana alizoeleka na alimjua Sakina vizuri sana.
“Nzuri Shikamoo”
“Marahaba,Mzee yupo?”
“Ndiyo”
Deo Karekezi akapiga hatua kumi na mbili ndipo akafikia kibaraza cha nyumba,akagonga.
“Hodi hodi”
“Karibuu Deo”
Mama Rebeca ndiye aliyeitikia,mlango ukafunguliwa wakasahabahiana na kupeana mikono.Kila mtu alionesha tabasamu na uchangamfu.Wakapita mpaka Seblen.
“Nilikuwa naangalia angalia tamthilia,chanel five.Hii Siri ya mtungi”
Mama Rebeca akaanza mazungumzo.
“Ni vizuri sana,haswa ukiwa umepumzika.Mimi kuangalia tivii mara chache sana”
“Kwanini?”
“Ubize,narudi nyumbani nimechoka, sanasana nitaangalia taarifa ya habari au movie”
“Sakinaaa”
Mama Rebeca kama kawaida,akamuita mfanyakazi wa ndani.
“Abee Mama”Akafika.
“Leta glasi na ile castle light kwenye friji”
“Sawa Mama”
Baada ya kutoa maagizo hayo akamgeukia Deo.
“Enhee Mwanangu,za masiku?”
“Salama tu Mama”
“Umetutupa mkono mwanangu,tangu uoe umekuwa kimnya inaelekea mkeo anakubana sana”
Mama Rebeca nayeye akaanzia mbali alitaka kuanza kumchimba Deo.
“Hapana Mama majukumu ndiyo yameongezeka tu”
“Vipi lakini familia haijambo?Marietha nimemmisi sana”
“Yupo sema amesafiri kidogo,Mama yake anaumwa”
Deo Karekezi aliongea akiwa mkavu bila kupepesa macho,ungeambiwa kwamba mwanaume huyu hapo alipo anazungumza uongo ungebisha.Kwa kuzuga akachukuwa glasi aliyoletewa na Sakina akainua na chupa ya bia akaanza kumimina kwenye glasi.
“Ahsante”
Akamwambia Sakina kwa nia ya kuzima mada!
“Anaumwa nini tena jamani?”
Mama Rebeca akauliza, bado alikuwa anataka kujuwa uongo wa Deo ungeishia wapi,ukweli ni kwamba alimficha Marietha chumbani kwa wakati huo.
“Mifupa,alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa huo muda kidogo na….”
“Oh Deo…”
Mzee Benjamin Ngowi akatokeza Seblen akitokea chumbani,Deo akasimama kwa adabu zote na kumsalimia kisha wakaketi kwa pamoja!
“Nilikuwa najimwagia maji kidogo”
“Wala usijali Mzee ndiyo nimefika sasa hivi, hata hivyo hapa ni nyumbani”
“Ni kweli kabisa”
Baada ya salamu za hapa na Pale Mzee Ngowi akaibua mada ya Marietha sababu hiyo ndiyo ilifanya mpaka amuite Deo nyumbani kwake.
“Mwenzako vipi?”
“Nani Marietha?”
“Ndio”
“Bado hajarudi”
“Atarudi lini kwani?”
“Nadhani wiki ijayo hapo”
“Alienda lini?”
Maswali yalikuwa mengi kwa Deo kama yupo kituo cha polisi hiyo ilimkera lakini hakutaka kulionesha swala hilo waziwazi.
“Majuzi hapa”
“Mara ya mwisho kuwasiliana naye lini?”
Deo badala ya kujibu swali akachukuwa glasi ya bia akapiga fundo moja refu kama kamba,akarudisha glasi juu ya stuli,alivyoulizwa swali lingine akaweka tena glasi mdomoni.Hiyo haikusaidia, aliendelea kunyeshewa mvua ya maswali.
“Marietha jana sijampata,simu yake haikuwa hewani,itakuwa mambo ya mtandao”
Mzee Benjamin Ngowi hakutaka kuuliza maswali mengine zaidi akasimama akaingia chumbani na alivyotokeza Seblen baada ya sekunde kumi alikuwa na Marietha pembeni.
Kitendo cha macho ya Deo kutuwa usoni mwa Marietha akashtuka kutokana na pombe kuwa kinywani,ikampalia akaanza kukohoa mfululizo.Alijisikia aibu sana kudanganya, hapohapo akaangalia chini.
“Deo,nini kinaendelea?”
Mzee Benjamin Ngowi akauliza huku akimtizama Deo,Marietha kwa wakati huo alikuwa akibubujikwa na machozi!



Mbele yake alikuwa amesimama Marietha akiwa na Mzee Ngowi, kwenye sofa ameketi Mama Rebeca,macho yote yapo kwake.Alihisi uti wake wa mgongo umepigwa na ubaridi wa ghafla sababu mambo aliyokuwa anaongea tayari yalikuwa wazi,alidanganya kwamba Marietha yupo na Mama yake mkoani anamuuguza.Vitu vingi vilipita ndani ya halmashauri ya kichwa chake.
“Deo,kuna nini?Naomba unieleze”
Mzee Ngowi akarudia tena swali lake alitaka kujuwa nini kinaendelea baina ya mtu na mkewe na alitaka kuwasuluisha siku hiyohiyo,kwa busara alizokuwa nazo alijuwa kwamba kila kitu kingekuwa sawa, jambo hilo kwake alilipa asilimia zote mia moja.Mpaka hapo Deo hakuwa na cha kujibu aliinamisha kichwa chake chini.
“Mzee wangu,wacha niongee ukweli”
Hatimaye akazungumza na kumtizama Marietha,kila mtu alitaka kumsikiliza hata Marietha vilevile alikuwa pembeni yake.
“Marietha amebadilika sana,ni mambo ya aibu kuyazungumza mbele yenu mnisamehe kwa kuwaambia amesafiri nilitaka nifiche hii aibu.Tangu nimuoe amekuwa akinionesha dhara…”
“De..o”
Marietha akaingilia mambo aliyokuwa anaongea Deo yalimshangaza mno.
“Nyamaza niseme uchafu uliokuwa unafanya,hivi unadhani mimi ningeweza kuvumilia?”
Deo akamnyamazisha Marietha kwa sauti ya ukali na sura yake tayari ilionesha makunyanzi kumaanisha kwamba amekasirika mno,alimtizama Marietha kwa macho makali sana kama chui.
“Samahani kwa kusema haya mbele yenu lakini leo imenibidi, Marietha ni Malaya.Amebadilika,ngoja niwaoneshe kitu”
Deo Karekezi akatoa simu yake moja kubwa mfukoni,akawa anabonyeza kisha kumsogezea Mzee Ngowi.
“Embu tizama”
Macho ya Mzee Ngowi yalituwa juu ya kioo cha simu ya Deo hata yeye alionekana kushtuka mno,picha za utupu za Marietha akiwa na mwanaume mwingine kitandani zilimshtua sana,akaangalia pembeni na kumsogezea simu mkewe,Haika nayeye akapitisha macho yake,Marietha alikuwa ndani ya shuka jeupe juu hana kitu yupo kifuani kwa mwanaume mwingine wamejifunika,picha hiyo hata angeoneshwa mtu mwenye utindio wa ubongo angeelewa nini kimetokea bila hata kupewa maelezo.
“Hii ni aibu kubwa,sio hiyo tu”
Deo akachukuwa tena simu akawa ana kazi ya kuonesha picha tofauti za Marietha tena akiwa na wanaume tofauti tofauti wakiwa katika pozi za ajabu za kimahaba.Marietha alikuwa pembeni hakuelewa ni kitu gani kinaendelea lakini alihisi kitu,akaomba simu na kupewa.
Moyo wake ukapiga paa! Akahisi kama mwili wake umepalalaizi ghafla,alizishangaa picha hizo sababu katika kompyuta yake ya kichwani inayohifadhi kumbukumbu haikumpa jibu sawasawa,hakuwahi kufanya kitu kama hicho katika maisha yake.Hakuelewa imekuwaje mpaka picha hizo zikatengenezwa,alimwaga machozi sababu kila aliposukuma picha nyingine alijiona yeye akiwa na wanaume wengine mbalimbali,moyo ulimuuma kupita kiasi na mpaka wakati huo hakuelewa aseme nini ili aaminike,ushahidi ulikuwepo wazi,alitamani Mungu ashuke awe shahidi yake sababu ndiye anayejuwa kila kitu.
“Hivi Marietha ulijiona wewe mjanja sana?nilikupenda sana.Lakini umenitenda umeniaibisha,kulikuwa na picha nyingi sana humu ndani ya simu nimezifuta sababu najisikia uchungu”
Deo alijifanya kuongea kwa simanzi huku akipiga piga kifua chake kwa uchungu.
“Inaniuma sana mzee wangu,mimi nimeshindwa,Ninampenda Marietha lakini kwa hili wacha nikajifikirie”
“De..o la..k..”
Marietha aliongea kwa kwikwi,kila alipotaka kusema kitu alishindwa kiungulia kilikuwa kimemkaba kohoni anatetemeka kwa hasira,alitamani amvae Deo amalize hasira zake lakini aliogopa kufanya hivyo.Ni kweli alikuwa amesingiziwa, isingewezekana hata kidogo kwa yeye kufanya kitendo kama hicho sababu alijiheshimu sana.
“Unataka kuongea nini?Unataka kuongea nini Marietha eeeh?Unataka kuongea nini kahaba wewe,mnafki mmoja mpuuzi.Ningejua nisingekuoa,sikujuwa kama nafuga nyoka mkubwa ndani ya nyumba yangu....Naongea nawewe Malaya,hivi ulidhani sitojuwa?”
Deo aliongea huku akitetemeka kwa hasira,akasimama na kusukumiza stuli ili amfuate Marietha amtandike makofi lakini kabla ya kumfikia Mzee Ngowi alisimama kama Mwanajeshi akamshika na kumzuia.
“Deo punguza jazba”
“Hapana nataka nimfunze adabu,niache nimpige makofi.Nilimnunulia gari zuri nilimjengea nyumba nzuri Mama yake mzazi lakini matokeo yake wote yeye na Mama yake washenzi wa tabia”
Deo alizidi kutoa matusi ya nguoni akawachanganya wote Marietha na Mama yake mzazi,alikuwa bado mikononi mwa Mzee Ngowi anajaribu kujitoa.
Mama Rebeca alikuwa kimnya haelewi akae upande upi,hakujuwa yupi mkweli yupi muongo.
“Mzee Ngowi kama umeniita kwa ajili ya Marietha naomba niende zangu na ninajuwa kawaambia maneno ya uwongo”
Deo akajihami,aliongea na kuchukuwa simu yake iliyokuwa juu ya stuli.
Akamtizama Marietha kwa macho makali mno tena ya hasira,akageuka bila kuaga na kutembea mpaka mlangoni, akaufungua na kutoka zake nje,akanyoosha mpaka nje ya geti akaingia ndani ya gari.Akawasha na kuligeuza alivyofika umbali wa kama mita kumi,akatabasamu kidogo na kushusha pumzi.
“Duu! Kumbe mimi ni msanii mkubwa sana,lazima nikaombe nafasi bongo movie nitaongea na JB Jacob Steven ama Vincent Kigosi,nina namba zao hapa”
Deo akajisemesha mwenyewe, mambo aliyofanya alijiona yeye bab kubwa sana,hapohapo akachukuwa simu yake, mkono mmoja ukiwa kwenye usukani na mwingine kashika simu,akawa anaangalia mbele huku anatafuta jina kwenye simu akaingia ‘search’ na kubonyeza herufi ‘G’majina yote yanayoanza na herufi hiyo yakatokeza juu ya kioo akashuka chini mpaka kwenye jina GIPSON PAUL,akairuhusu simu itoke na kuiweka sikioni.
“Yes Halloo Gipson,uko wapi? Kazi imeenda vizuri.Upo wapi?Studio?”Okay sawa tukutane hapo Tabata Matumbi,mimi natokea kinondoni,nikifika hapo nitakupigia”
Simu ikakatwa.
Gipson Paul alikuwa ni kijana mdogo lakini mtundu kwenye mambo ya ‘graphics design’huyu ndiye Deo alimsaka usiku kucha ili kutengeneza picha chafu za utupu za Marietha,alijuwa kivyovyote vile ni lazima angeulizwa kuhusu ugomvi wake na Mkewe ndiyo maana akajihami ni kweli alikuwa ni kama ametabiri siku hiyo hata alivyopigiwa simu na Mzee Ngowi alichezwa na machale sababu ilikuwa ni lazima Marietha angewatafuta watu wake wa karibu,swala lake likazaa matunda.
Akazidi kunyoosha mguu na kuingia barabara ya Magomeni,akatembeza gari mpaka Manzese Tiptop akakunja kona ya kuelekea Mabibo,alitaka afupishe njia atokee Tabata ili aonane na Gipson Paul,akaipita Mahakama ya ndizi.Alikuwa makini juu ya usukani vidole vyake anavichezesha na kutingisha kichwa,mziki uliokuwa ndani ya gari ulimburudisha.Alivyofika Mabibo mwisho akakutana na njia panda,akaangalia magari vizuri akakunja kulia na kunyoosha mpaka Ubungo maziwa shungashunga,akakunja kushoto.
Baada ya dakika tatu akatokeza External,akasimama sababu taa nyekundu zilikuwa zinawaka.
“Griii griiii”
Simu ndiyo ilimshtua akaangalia juu ya kioo,namba ilikuwa ngeni akaitizama kwa kitambo kidogo.Alivyotaka kuichukuwa taa za kijani zikawaka,akaweka gia na kuchomoka ambapo alizungusha usukani kushoto na kuingia ‘high way’.Nusu saa baadaye alikuwa Matumbi akaweka gari kando na kumtafuta Gipson Paul hewani ili ampe fungu lake kwa kazi nzuri aliyofanya!
***
Leila alikuwa ameinama ameshika magoti yake,nyuma yake alisimama Rashid Tengeza kama Ngongoti mikono yake ipo kiunoni kwa Leila,kiuno chake kinarudi nyuma na kwenda mbele tena kwa mwendo wa spidi mia saba,kazi ya Leila ilikuwa ni kutoa miguno ya ajabu sababu ilionekana nyoka aliyeingia shimoni mwake alipenya mpaka ukingoni ndiyo maana nayeye alinyonga kiuno taratibu, utamu ulikuwa umekolea barabara!
Jinsi alivyokunjwa ilitishia amani, hakuwahi kufanyiwa kitu kama hicho maishani mwake.Nyoka akiwa ndani ya shimo hivyo hivyo akainuliwa juu juu,Tengeza akamgeuza kiufundi wakawa wanatizamana mikono ya Leila kaiviringisha shingoni mwa Tengeza,miguu yake alkadhalika kaiviringisha kiunoni mwake,akawa yupo hewani,Tengeza akachukuwa mikono yake akashika makalio vizuri ili impe nafasi nzuri mambo yakaanza upya,wakaendelea kupigana madenda huku chini wakinyonga viuno vyao.Zoezi hilo lilidumu kwa takribani dakika mbili nzima,Puu! Leila akatupwa kitandani,Rashindi Tengeza akapanda juu yake,akachukuwa mguu wa Leila wa kushoto akauweka begani kwake,akamtumbukiza tena nyoka wake ndani,mashambulizi yakaendelea.
****
Dunia siyo mbaya,siku zote walimwengu ndiyo wabaya.Bado mpaka wakati huo alidhani yupo ndotoni anaota ndoto ya kutisha,hakuna siku ambayo hatokuja kuisahau katika maisha yake kama hiyo.Mwanaume aliyempa mimba leo hii amemtelekeza anamuita Malaya,mbali na hapo aligushi picha ili kusindikizia uwongo wake.
Ulikuwa ni udhalilishaji wa hali ya juu,hakuelewa mpaka wakati huo Mzee Ngowi na Mkewe wanamfikiria vipi ndiyo maana alipanga usiku mnene ukiingia atoroke ili akimbie aibu,hakuelewa siku itakayofuata atawaangalia vipi watu hao usoni,ilikuwa ni aibu ya mwaka.
Tumbo lake lilikuwa kubwa tayari na aliamini kwamba muda mchache ni lazima atajifungua.
Alikuwa chumbani akizidi kulia machozi.Maneno ya Deo yalikuwa yakimpitia kichwani kwake,akajaribu kuyalinganisha na mambo yalitokea nyuma,akamuona Leila anavyoingia nyumbani kwake,akapigwa kipigo cha mbwa mwizi,hilo ndilo lilimfanya aumie mtima zaidi!Kwa maana hiyo hakutaka tena kuendelea kubaki ndani ya nyumba ya Mzee Ngowi ingawa walimwambia abaki nyumbani hapo,akajikita kwenye mawazo.
Akasubiri mpaka alivyohisi umekuwa usiku mnene,taratibu akaanza kunyata,akafungua mlango na kutoka nje.Akapita mpaka seblen.
“Marietha vipi?”
Sauti ya Sakina ndiyo iliyomshtua,alikuwa seblen anaangalia televisheni sinema ya ngono lakini kwa sauti ya chini.
“Maji ya kunywa,natafuta maji ya kunywa”
Hakutaka kusema hila zake ndiyo maana akazuga,Sakina akazima luninga akatembea mpaka jikoni na kumkabidhi Marietha kikombe cha maji,akanywa bila kupenda kisha kurudi chumbani kwake,kitendo cha kuweka mwili wake kitandani usingizi ulimchukuwa hapohapo.
***
Anga ilikuwa nzito na kulikuwa na giza nene,na usiku huo ulikuwa kama mchana kwa watu wengine. Babu Kinyogoli alikuwa juu ya ungo na wenzake watatu wapo angani huo ndio ulikuwa usafiri wao kila siku na walikuwa uchi wa mnyama,safari yao ilikuwa ni kwa Marietha ilikuwa ni lazima waitoe mimba yake kama walivyomuhaidi Leila,hilo waliapia kulifanya siku hiyo ndiyo maana walimfungia safari.
Mikononi walishika usinga wenye manyoya na vichwani walifunga vitambaa vyeusi.Ndani ya sekunde tisa walitua juu ya paa la Mzee Ngowi kitu cha kwanza kukifanya ni kumimina dawa aina ya nywinywila nyumba nzima, kazi ya dawa hiyo ilikuwa ni kumfanya binadamu alale na kuota ndoto nzuri,wakatua chini na mmoja mmoja akaanza kuingia ndani kwa staili ya kutumia makalio,mpaka wote walivyoingia ndani ya chumba cha Marietha,Babu Kinyogoli ambaye alionekana ni mkuu wao akatembea mpaka kwa Marietha aliyekuwa kitandani amelala,akamuwekea Kibuyu juu ya tumbo lake.
“Ashamtu ashamtu,bruchachaa..Arapatata”
Babu Kinyogoli alikuwa anaongea maneno yake ya kichawi,akachukuwa usinga na kuanza kumpiga nao Marietha usoni.
“Fyaaa fyaaaa”
Marietha akapiga chafya akiwa bado usingizini,hakuelewa chochote kile.Wachawi waliendelea kumchezea.
“Ng’aaaa! ng’aaaa! ng’aaaaaa!”
Sauti ya mtoto mchanga ikaanza kusikika chumbani,Babu Kinyogoli akatabasamu akazidi kufanya uchawi wake.
“Nyauuuu nyaaaauuuu”
Sauti za paka zikaanza kusikika hiyo ilimaanisha kwamba uchawi wao unafanya kazi na baadaye bundi walianza kulia,tumbo la Marietha likaanza kupakwa dawa nyeusi,nguo yake ikapandishwa juu,akanyunyiziwa mafuta ya kondoo tumboni yaliyokuwa ndani ya kichupa cheusi.



“Nisaidiee,Nisaidieni jamaaani. Wataniua,nisaidieni”
Alikuwa yupo katikati ya kundi la watu anaomba msaada lakini watu hawakumjali,walimuangalia na kumpita kando.Tumbo lake lilikuwa kubwa na alishindwa kukimbia, alikuwa amechoka kupita kiasi.
“Kaka naomba unisaidie wanataka kuniua”
Marietha alizidi kuomba msaada nyuma yake kulikuwa na watu wanamfuata wameshika mapanga, sura zao zilikuwa za ajabu sana tena walikuwa mita chache nyuma yake,hofu ilizidi kumtanda akazidi kusonga mbele ambapo aliona kuna njia nyembamba akaingia na kujificha ili asionekane,alivyoona sehemu hiyo sio salama kwake akasimama ili aendelee na safari.Tumbo lake lilianza kumuuma mno,akalishika kizunguzungu kikali kikamvaa akahisi anaishiwa nguvu,hapohapo akadondoka chini.Kwa mbali aliwaona watu wanaomfuata wameshika visu na mapanga wakamfikia,usoni walikuwa wameziba sura zao.Mmoja akavua kitambaa alichojifunga usoni.
“Le..ila tafadhali usiniue”
Alikuwa ni Leila amesimama mbele yake yuko na wazee wengine watatu pembeni yake wamevaa nguo nyeusi.
“Lazima nikutoboe tumbo lako”
“Ha..pana Lei..la usifanye hivyo”
“Siwezi kukuacha uwe hivi,mzee fanya kazi yako”
Mzee mmoja aliyeshika panga akasogea karibu na Marietha akainua panga juu,maana kwamba angelishusha basi utumbo wa Marietha ungemwagika chini.Kwa hali ya kushangaza ukatokea mwanga mkali mweupe sana ukamulika kila mahali,Leila na wazee waliokuwa kandokando yake wakadondoka chini chali.Miale ya mwanga huo ilikuwa mikali kupita kiasi,haikuwa rahisi kuona mbele lakini kadri sekunde zilivyozidi kusogea mwanga ulikuwa ukipungua.
“Mariethaaa,Usioogoope”
Sauti hiyo ilisikika kama mwangwi ikijirudia rudia.Marietha alitandwa na hofu alivyogeuza shingo yake pembeni alimuona Mwanamke mzuri amevaa nguo nyeupe mithili ya shela la harusi lakini mgongoni alikuwa ana mabawa alikua akiwaka mwili mzima,hakutaka kulipitisha swala hilo kichwani kwake kwamba mtu huyo ni malaika.
“Shika hii,Sali sana Muombe Mungu nayeye atakusaidia”
Mwanamke huyo aliyefanana na Malaika alikambidhi Marietha Biblia kisha akapotea.
***
Marietha alikurupuka kitandani asubuhi ya saa kumi na moja,kulikuwa tayari kumepambazuka. Ndoto aliyoota alishindwa kuielewa kama ni kweli ama ni maono,alijivuta kwa juu na kukaa kitako akaligusa tumbo lake ambalo bado lilikuwa kubwa,majasho yalikuwa yakimtiririka mwilini,hakuelewa yalitokana na nini,alihisi mwili wake umechoka kuliko siku zote.Mpaka hapo hakupata usingizi hata kidogo mpaka inafika asubuhi ya saa kumi na mbili.Kitendo cha kuweka mguu juu ya malumalu alihisi maumivu yasiyo ya kawaida,nyonga zilikuwa zinavuta alivyojitahidi kusimama ilikuwa ndio kama anazidisha maumivu.
Maumivu yakazidi kuwa makali,kilichomchanganya zaidi ni baada ya kuangalia juu ya shuka,macho yalimtoka moyo wake ukawa unapiga kwa nguvu huku maumivu yakizidi kuendelea.
“Sakinaaaaa!”
Akaita kwa sauti ili apatiwe msaada lakini hiyo haikusaidia kuzuia maji yanayomtoka na kuzidi kulowanisha shuka.
“Sakinaaaa”Akaita tena huku akipiga piga mapaja yake.
Mfanyakazi wa ndani hakuwa ana habari yoyote alikuwa uwani anafua huku ameweka ‘headset’ masikioni mwake hakuelewa kwamba ndani Marietha anapiga kelele anaomba msaada wake.
Ni kama Mungu vile siku hiyo Mama Rebeca aliamka asubuhi na mapema ilikuwa ni kama malaika alimuamsha akatoe msaada sababu Mama huyo hakuwahi hata siku moja kuamka asubuhi na mapema kiasi hicho.
“Saakinaaaa”
Mama Rebeca aliyekuwa anatokeza mlangoni alisikia kelele za Marietha,akaanza kutembea harakaharaka, akanyonga kitasa cha mlango wa chumba anacholala Marietha,alichokiona kilimshtua,akarudi kwa kasi ya mkuki mpaka kwa mumewe.
“Baba Rebeca,Baba Rebecca”
Staili aliyotumia kumuamsha Mumewe ilitisha,alikuwa ni kama mtu anayeunguliwa na nyumba.
“Nini?Vipi?Kuna nini?”Mzee Ngowi alikurupuka kama mgambo aliyemwagiwa maji akiwa lindoni anasinzia.
“Chupa ya Marietha imepasuka,vaa tumpeleke hospitali”
“Mungu wangu unasemaje?”
“Vaa Baba Rebeca”
Mzee Benjamin Ngowi akatoka ndani ya shuka na kurukia bukta yake kabatini,akavuta na shati hata kabla ya kufunga vifungo akaingia mpaka chumbani kwa Marietha,maji yalikuwa yanaendelea kumtoka.
“Sakinaaaaaaaaaaa”
Sauti ya Mama Rebeca ilikuwa kali mno ingawa Sakina aliweka mziki mpaka mwisho lakini ilimfikia akiwa uwani anafua,akaweka simu pembeni na kuvua ‘headset’ masikioni.
“Abee Mama”
Akaitikia huku akijipangusa mikono iliyokuwa na mapovu akaingia mpaka ndani,butwaa alilopigwa halikuwa na kipimo chake.
“Mshike Marietha mkono huo huko”
Marietha alikuwa katikati ya Mama Rebeca na Sakina, wakasaidiana mpaka nje ambapo Mzee Ngowi alikuwa tayari yupo ndani ya gari anarudisha nyuma,akaliweka sawa.
Wakamuingiza ndani ya gari.
“Sakina baki linda nyumba sisi tunakuja,sawa?Na usisahau kufunga geti”
Mama akatoa maagizo huku akiingia ndani ya gari.
“Sawa Mama”
Mzee Benjamin Ngowi akapiga gia akachomoa gari kwa kasi alimanusura agonge ukuta,akaingia barabarani na kunyoosha mguu,ilikuwa ni asubuhi na mapema hivyo magari hayakuwa mengi barabarani.
Marietha alikuwa akipiga kelele ndani ya gari, alibanwa na uchungu wa kuzaa hiyo ilimchanganya sana Mama Rebeca na Mumewe.Hawakuchukuwa hata dakika ishirini wakawa wameingia ndani ya geti la hospitali,kabla ya kuzima gari Mzee Ngowi akashuka kwa kasi mpaka mapokezi.
“Nesi ninahitaji msaada kidogo,kuna mjamzito huku”
Wauguzi na wao walikuwa kama wanajeshi wakatoka na kiti chenye matairi chini mkuku mkuku mpaka kwenye gari,wakamtoa Marietha na kumuweka juu ya kiti,wakaanza kukisukuma kiti.
Baada ya taratibu zote kukamilika wakamuingiza moja kwa moja chumba maalum cha wanawake wanaojifungua yaani ‘labour room’wakampandisha mpaka juu ya kitanda.Miguu yake akaipanua huku na kule,Manesi walikuwa tayari wapo kandokando wanapigana vikumbo mara washike hiki mara kile.
“Utajifungua salama,bana pumzi.Nikisema sukuma unabana pumzi unasukuma.Moja mbili tatu.Sukuma”
Marietha alikuwa anatokwa na majasho, maumivu ya uchungu wa kuzaa yalikuwa makali,lakini alijikakamua.
“Sukumaa”
Manesi wakazidi kumsihi afanye hivyo,Marietha akajitahidi kufanya hivyo.
“Kichwa kipo nje,jitahidi Mama,Jitahidi mtoto anatoka jitahidi sukuma usiache.Sukuma tena usiache”
Ni kweli kichwa cha mtoto kilianza kutangulia, Nesi mmoja alikinga mkono wake ili kumpokea kutoka mlangoni,Marietha alizidi kufanya alichoagizwa alijitahidi mno.
“Ng’aaaa ng’aaaaa ng’aaaaaa.Hongera sana ni mtoto wa Kiume”
Ingawa alikuwa amechoka lakini alionesha tabasamu usoni,akawekewa mtoto kifuani mwake akamshika vizuri huku akilia machozi ya furaha,bado hakuamini kwamba mtoto aliyekuwa juu yake amemzaa yeye!
***
“Hapana nenda tu,hatuwezi kukusaidia tena.Kama kuhusu huyo Marietha sisi tumemshindwa Mzee anaumwa sana,amezidiwa”
“Tafadhali nisaidie”
“Nenda labda siku nyingine,yule mwanamke ana nguvu za ajabu.Nenda kwanza”
Leila alikuwa kilingeni,ndani ya chumba cha mganga wa kienyeji, alitaka kupata majibu ya Marietha kuhusu mimba yake imefikia wapi,majibu aliyopewa yalimvunja moyo yakamkata maini.Kushindwa kwa waganga hao kutoa mimba ya Marietha kulimfanya adate,akashindwa kuelewa ni kitu gani kilitokea mpaka waganga hao ambao walikuwa bingwa kushindwa.
Ni kweli usiku uliopita ilikuwa kidogo wapoteze roho zao sababu walipigwa na radi na wote kudondoka chini chali,hawakuelewa nguvu za Marietha zilitokana na nini hapo ndipo waliamua kupotea na tangu siku hiyo Babu Kinyogoli aliumwa vibaya sana.
“Toka bwana”
Mzee ambaye alikuwa msaidizi wa Babu Kinyogoli alifoka kwa ukali,Leila akasimama na kuondoka zake, ambapo alitembea mpaka alipoegesha gari na kulirudisha kinyume nyume,alipokaa sawa akaondoka zake huku kichwani akiwa mwenye mawazo lita mia moja.
****
“Unasemaje?Pesa haitoshi?Kivipi?”
“Ndio bosi pesa haitoshi”
“Fafanua,kivipi wewe?Wakati juzi Violeth Ndoss aliniambia kuna milioni mbili kwenye mauzo”
“Ndio zilikuwepo,alikuja hapa kuchukuwa pesa juzi”
“Nani?”
“Leila”
“Niniii?”
Deo alisimama akapiga meza kwa hasira makaratasi yakaruka,sura yake ilikuwa tayari imejikunja ilikuwa ni asubuhi na mapema, siku yake tayari ilikuwa imeharibika.
“Kachukuwa kiasi gani?”Akauliza tena.
“Kachukuwa pesa zote”
“Unasemajeeeee?”
Deo aliuliza kwa sauti iliyosindikizwa na hasira za waziwazi,alikasirika ajabu.Pesa za mauzo alizokuwa anategemea kununua mzigo mwingine wa biashara ili auzungushe zilichukuliwa na Leila tayari.
Hapohapo akachukuwa simu ya mkononi,akatafuta namba za Leila akapiga,akaweka simu sikioni akiwa anahema kwa hasira.
“Uko wapi?”
Hilo ndilo swali la kwanza kuuliza Deo baada ya simu kupokelewa upande wa pili.
“Vipi Deo mbona unaniuliza kwa sauti ya juu,kuna ni…?”
“Nakuuliza upo wapi?”
“Naendesha gari”
“Unaendesha gari?Unaenda wapi sasa hivi asubuhi?Nani kakuruhusu uje kuchukuwa pesa hapa ofisini bila ruksa yangu?”
“Lakini baby ni..”
“Don’t call me baby,pesa ziko wapi?hizo pesa nataka urudishe sasa hi…tititi”
Simu hapohapo ilikatwa,Deo alivyojaribu kuipiga tena namba haikupatikana Leila alimzimia simu, mbele yake bado alikuwa amesimama sekretari wake Ruth Edson,anatetemeka hakuwahi kumuona bosi wake amekasirika kiasi hicho.
“Nani alimpatia hizo pesa?”
“Abee Abee bosi ni Nancy”
“Mwite”
“Abee”
“Mwiteeeee”
Deo akafoka kwa sauti,alitetemeka kwa hasira hiyo ilifanya mpaka sauti yake ipenye nje wafanyakazi wake wakasikia.Ruth Edson akavuta mlango na kutoka nje,akaingia mpaka ofisi ya ‘cashier’.
“Nancy unaitwa”
Akasema baada ya kufika mezani kwa msichana mwingine wa makamo huyu alikuwa mtu wa ‘accounts’mahesabu yote ya kampuni ilikuwa ni lazima afikishiwe Nancy,alivyosikia hivyo mkojo ulitaka kumtoka,akasimama na kuweka sketi yake vizuri.
“Ruth”
Nancy akamuita mwenzake.
“Vipi?”
“Kuna nini?”
“Mimi sijui,bosi anakuita.Tena uende sasa hivi”
Nancy alikuwa msichana mwoga pengine kuliko mfanyakazi yoyote yule,alimuogopa tajiri yake kama ukoma ndiyo maana alianza kujishauri ni kipi Deo anamuitia asubuhi yote hiyo ingawa alianza kuhisi,akatoka ofisini kwake mpaka mlango wa bosi wake,akapiga ishara ya msalaba kutokana na hofu,akasukuma mlango wa kioo.Sura aliyoiona mbele yake ilimtisha.Deo alikuwa amesimama kama mlingoti, macho mekundu.
“Mimi na Leila nani bosi wako?”
Lilikuwa ni swali alilotupa Deo akimtizama Nancy machoni kwa hasira.
“Nakuuliza mimi na Leila nani bosi wako?”
“Ni ni ni wewe hapo ndio bosi wangu”
“Nani kakupa ruksa ya wewe kumpa pesa bila mimi kutoa ridhaa yangu?”
Lilikuwa ni swali lingine kutoka kwa Deo tena likisindikizwa na sauti ya ukali.
“Alikuja hapa aliniambia kwamba wewe ulimruhusu”
“Kwanini hukunipigia simu kuniuliza?Kwahiyo mtu yoyote akija kutaka pesa unatoa?”
“Hapana bosi”
“You know what,you are fired.Full stop”(Unajua nini nimekufukuza kazi.Nukta)
Kutokana na uzembe wa kutoa pesa bila ridhaa ya tajiri yake,Nancy akawa amepoteza kazi yake,alidondoka chini kwa magoti huku akimwaga machozi.
“Nimekufukuza kazi,nitokee ofisini kwangu upesi”
“Bo…si naa..ombaa”
Nancy alililia msamaha.
“Griii griiiii”
Simu ya Deo ilianza kuita ikiwa mezani kwake, alivyoangalia aliona jina MRS.Ngowi akasubiri kwa muda na kutafakari,hakuelewa aipokee ama aipotezee, alijuwa kabisa zilikuwa ni habari za Marietha kuombewa msamaha.Akaichukuwa simu,akaipokea na kuiweka sikioni.
“Halloo Mama shikamoo,kama kuhusu Marietha tafadhali,siwezi kumsamehee”
Deo alianza kuongea harakaharaka bila breki.
“Hongera Deo mkeo amejifungua mtoto wa kiume”
Sauti kutoka kwa Mama Rebeca ilisikika upande wa pili wa simu,hiyo ilimfanya Deo agande kama barafu!


Sio kwamba hakusikia kile anachoambiwa bali maneno yaliyopita masikioni mwake yalikuwa kama yamemzindua kutoka usingizi wa kifo,mawazo yake yakarudi nyuma kwa kasi ya mwewe.Akajiona alivyokuwa anamtesa mkewe, akampiga nusura kumuuwa kabisa tena akiwa mjamzito jambo ambalo alikuwa akilitaka kwa muda mrefu sana,alijiona kama mkosaji mbele za Mungu sio siri kuna kitu alianza kukihisi kwamba hazikuwa akili zake hata kidogo.
“Mpo mpo mpo hospitali gani?”
Deo akarudi tena kwenye laini baada ya kutafakari kwa muda mrefu kidogo.
“Kwa Dokta Yuditha Ngopi Kinondoni B”
Jina la mwanamke huyo daktari halikuwa ngeni katika masikio yake ingawa hakuwahi kufika katika hospitali hiyo kupatiwa matibabu.
“Sawa,ahsante ninakuja”
Hatimaye simu ikakatwa Deo akakusha pumzi ndefu ya ndani kwa ndani.Alitamani kuvaa koti lake na kwenda hospitalini kumuona mke wake lakini alishindwa,aliona aibu mno.
Hakuelewa atamuangalia vipi Marietha usoni.Kwa matendo aliyomfanyia alistaili adhabu kali kuliko hata ya kuchomwa na moto wa shetani.Alikuwa mbali sana kimawazo,akainamisha kichwa chake na kukiweka juu ya meza.
“Ngo ngo ngo”
Mlango wake wa ofisini ukagongwa.
“Ingia”
Akasema huku bado kichwa kikiwa bado juu ya meza.
“Sema”Akazungumza.
Hakujua ni nani amesimama ofisini kwake,kichwa chake kilijaa mawazo kikawa kizito kuinuka.
“Bosi”
Ruth Edson mmoja wa wafanyakzi wake ndiye alikuwa mbele ya meza ya tajiri yake mkononi kashika mafaili,alikuwa akimsubiri bosi wake ainue kichwa ndio aseme shida yake.
“Bosi”
Akaita tena.
“Nakusikia Ruth sema”
“Kuna mafaili hapa un…”
“Weka hapo mezani”
“Lakini bosi upo sawa?”
“Weka mafaili mezani,kaendelee na kazi”
Bado kichwa cha Deo kilikuwa chini tu.Ruth Edson akamtizama Bosi wake, alitamani kujuwa nini kinamsumbua tajiri yake lakini majibu aliyopewa yalimkata maini,akageuza na kuondoka zake huku nyuma akimuacha Deo akiwa vilevile.
Sio siri alikuwa ni kama mtu aliyepararaizi ubongo, bado akili yake ilishindwa kuelewa ni kitu gani ifanye.Ghafla akapata wazo hapohapo,akainua kichwa chake na kuchukuwa simu yake iliyokuwa mezani.Akaanza kutafuta namba fulani kisha kuzipiga,akaweka simu sikioni ili kusubiri mtu wa upande wa pili apokee.
“Haloo Mr.Mtui,habari yako?”
Deo akaanza mazungumzo baada ya simu kupokelewa.
“Yes Deo,salama tu”
“Naweza kuonana nawewe?”
“Sasa hivi?”
“Kama ikiwezekana”
“Sasa hivi nipo kazini,labda jioni”
“No Mtui tafadhali nakuomba”
“Deo kuna nini?”
“Naomba nikuone nina matatizo”
“Wapi tuonane?”
“Popote wewe sema”
“Nitakuja posta sababu nilikuwa nina mpango huo”
“Ahsante sana,naomba umwambie na Msangi pia awepo”
“Okay”
“Shukrani”
Deo akakata simu,niya ya kuwaita marafiki zake ilikuwa ni kuwaeleza kila kitu na kuwaomba ushauri ni kitu gani akifanye,sio tu aliogopa kwenda kumuona Marietha alimuhofia pia Mzee Ngowi, hakuelewa itakuwaje akionana naye,kila alichokifanya alikijutia ndiyo maana alitaka kuwashirikisha marafiki zake wenye busara ili wampe ushauri.
***
Wa kwanza kufika ndani ya mgahawa wa ‘Chiken inn’mtaa wa samora avenue ni Deo,alikuwa ana hamu sana ya kuwaambia marafiki zake Mtui na Msangi jinsi mambo yalivyoenda ili wampe ushauri juu ya kitu gani akifanye.
“Dada niongezee juice”
Deo akaagiza juisi nyingine,ikaletwa kazi yake ilikuwa ni kuivuta kutoka kwenye mrija ili asukume mda.Alivyochungulia nje akaona gari ya Mtui inapaki,akatabasamu sababu ndani ya gari hilo pia alishuka Msangi.
“Mtui,nipo hapa”
Deo akapaza sauti alivyoona marafiki zake wanaangaza huku na kule.
“Vipi bwana Deo”
“Safi karibuni…Wewe dada leta juisi na sambusa”
Deo akawaagizia marafiki zake kwa bili yake mwenyewe,vinywaji na sambusa zilipowekwa mezani Deo akaanza mazungumzo.
“Kuna kitu kinanisumbua sana,ningependa mnishauri”
“Kitu gani hiko?”
Msangi akauliza.
“Ni kuhusu nini?”
Mtui naye akapata kihoro cha kutaka kujuwa,wote wakawa wanamwangalia Deo machoni.
“Mwenzenu nina majanga”
“Majanga?Majanga gani?”
“Ni kuhusu Mke wangu Marietha,amejifungua”
“Eh,hongera sana Deo Karekezi.Sasa ushampa mtoto jina?Ebwana hongera sana”
Msangi akaongea kwa furaha akimpongeza rafiki yake kipenzi kwa kuwa baba.
“Sasa mbona upo hivyo?inakupaswa ufurahi”
Mtui akatia neno.
“Sio kama mnavyofikiria?”
“Kumbe?Changa la macho nini?Mtoto sio wako,au?”
“Bora ingekuwa hivyo”
“Sasa kuna nini Deo?”
“Marietha nilimfukuza nyumbani kwangu,sasa hivi nina mwanamke mwingine mbaya zaidi nilimfanyia vitendo visivyofaa”
Deo akaanza kutiririka kila kitu,kuanzia mwanzo mpaka mwisho wala hakuficha kitu chochote kile kilichokuwa ndani ya kifua chake, alifanya hivyo sababu alihitaji ushauri kutoka kwa marafiki zake juu ya kitu gani akifanye.Deo alikuwa ni kama mtu anayesimulia sinema fulani ya kuuzunisha ambayo ilitizamwa na Mtui pamoja na Msangi,wote walibaki vinywa wazi,walishindwa kumuelewa Deo anayoyaongea ni kweli ama anawasimulia hadithi tu za akina Hussein O. Molito.
“Deo!”
Mtui akaita kwa mshangao.
“Nahitaji msaada wako rafiki yangu”
“Msaada gani wewe ni mnyama?hivi una akili wewe?”
Mtui akaongea kwa ukali kidogo,jambo hilo lilimtia hasira.
“Mtui sikiliza,nachohitaji kutoka kwako ni ushauri”
“Sasa ushauri gani kutoka kwetu?huo ushauri gani wakati ushavurunda”
“Japo kwenda hospitali kwenda kumuona muongee nae”
“Upuuzi huo”
Msangi nayeye akaweka neno lake,nayeye aliguswa na mkasa huo, alimuonea sana huruma Marietha,kitendo alichofanya Deo kilikuwa ni cha kinyama.
“Yaani unamfanyia Mkeo mambo ya kinyama kiasi hicho?No way,umemfukuza mpaka Mama yake kwenye nyumba uliyomjengea,ukaona haitoshi mpaka ndugu zako.Hivi Deo una akili wewe?au una laana”
“Nisikilizeni Mtui na Msangi”
“No,hiyo sio kazi yetu ni kazi ya mshenga wako.Hivi Deo wewe wa kumpiga Marietha?alafu unasema alikuwa mjamzito.Leo unasema twende tukamuone,labda Mtui sio mimi”
Mtui na Msangi hawakutaka kusikiliza upuuzi wa Deo,wakasimama na kuondoka zao.
“Nisikilize nikwambie Deo”
Msangi akarudi mezani kwa Deo.
“Kama utanifuta urafiki kwa ajili ya hili sawa,ila mimi binafsi siwezi hata kidogo.Tafuta mshenga wako au watu wengine”
Msangi alihitimisha na kutoka zake nje,akaingia ndani ya gari kisha wakaondoka zao wakimuacha Deo akiwa mwenye mawazo mengi kichwani,mpaka gari lao linaondoka bado aliendelea kulisindikiza kwa macho.
****
“Naomba simu niongee na Mama yangu”
Marietha alikuwa kitanda cha hospitali bado,pembeni yupo mwanaye mchanga,mbele yake walisimama Mzee Ngowi na mkewe, Haika.
“Naomba mtoto nim-bebe”
Haika akaomba mtoto ,akapewa.Alikuwa mwenye furaha kupita kiasi.Mzee Ngowi akatowa simu na kumkabidhi Marietha lakini moyoni Marietha bado alihisi uchungu ajabu.Bado aliendelea kuyatafakari maneno ya Deo na picha chafu za utupu akiwa na wanaume wengine kitandani!
Kila alivyokumbuka vitu hivyo aliumia mtima,aliona aibu mpaka kuwaangalia Mzee Ngowi na Mkewe usoni.
Alivyokabidhiwa simu alianza kubonyeza namba fulani,namba za mama yake alikuwa nazo kichwani.Akaweka simu sikioni ili kusubiri upande wa pili,simu ilikuwa ikiita lakini haikupokelewa.Akajaribu tena na tena.Ikapokelewa.
“Halloo Mama,Mimi Marietha ushafika tayari?Nimejifungua tayari”
Marietha aliongea bila breki lakini upande wa pili ulikuwa kimnya,hakuna mtu aliyejibu.
Lakini alichosikia kwa mbali kilimuogopesha.
“Halloo”
Akaongea tena.
“Marietha unaongea na Mjomba wako Lucas,Mama yako amefariki dunia leo asubuhi!”


*******
ENDELEA KUSOMA HADITHI NA SIMULIZI ZA MTUNZI….EMMANUEL F.KWAY(THE STORY MASTER)

0 comments:

Post a Comment

BLOG