Search This Blog

Sunday, May 31, 2020

BEDROOM PROFESSIONALS SEHEMU YA 7/10



BEDROOM PROFESSIONALS
MTUNZI….EMMANUEL F.KWAY(THE STORY MASTER)
AGE…(18+)
WatsApp…+255718 862176
SEHEMU YA 7 KATI YA 10 MWISHO
*******


Mama Katrina ama Dokta Khalia,alichanganyikiwa na hiyo ilionekana waziwazi tena mbele za watu
mbali na hapo ilikuwa ni siku ambayo isingejirudia katika maisha yake yote,ilikuwa ni siku ambayo mtoto wake wa pekee anafunga ndoa ndiyo majanga hayo yakatokea.Lilikuwa ni tukio lililofanya mashekh na maimamu watoke nje ya msikiti sababu wageni waalikwa wote walikimbilia nje wakitaka kujua nini kimetokea.Mfano ingetokea Dokta Khaila angechukuliwa vipimo vya Scania basi majibu yangetoka na kuonesha kuwa akili yake haipo sawasawa na ingeamriwa apelekwe milembe dakika hiyohiyo.Kujazana kwa watu na kuuliza haikusaidia chochote kwani Katrina alikuwa chini ajitingishi.
“Kuna nini?”
Mzee mmoja aliuliza baada ya kutoka nje msikitini.
“Katrina kadondoka”
“Kadondoka?Kivipi?Yuko wapi?”
“Ndio yupo pale katikati”
“Imekuaje?”
“Sijui kwa kweli”
Mpaka wanamuinua Katrina na kumpakia ndani ya gari walishapoteza dakika tatu nzima.
“Twende aghakhan tafadhali”
Dokta Khaila akatoa pendekezo hilo huku akiwa anahema kwa wasiwasi mwingi akimwangalia mwanaye kama anapumua,akapitisha kiganja chake juu ya pua za Katrina na kushusha pumzi ndefu baada ya kuhisi vidole vyake vinapulizwa na hewa kutoka puani mwa Katrina kumaanisha kwamba kuna uhai.
“Mpigie Khan,waulize wamefika wapi”
“Sawa Mama”
Zilikuwa asilimia tisini kuwa siku hiyo hakuna harusi tena kutokana na mambo yalivyoenda,bibi harusi na bwana harusi wamepoteza fahamu,kila mtu alikuwa katika kitendawili kikubwa.Minong’ono ya chini kwa chini ilianza kusikika kuwa nyuma ya tukio hilo kuna ndumba.
“Nahisi kuna uchawi hapa”
“Kwanini?”
“wewe bibi harusi na bwana harusi wadondoke,ulishawahi kuona wapi kitu kama hiko?Hapa kuna namna”
“Wewe nawee,umekalia tu imani potofu”
“Mimi nakwambia Mustapha,hapo kuna kizizi”
“Unachokiongea kuwa na uhakika nacho.Usipende kuhisi wala kushabikia vitu usivyovijua.Vitu vingine sio vya kuropoka Ujuwe, utakuja kufungwa bure”
“Sasa si naongea ukweli”
“Nenda bwana,niache kwanza hapa nina stress,nimechanga pesa nyingi ujuwe kwenye harusi”
Baadhi ya wageni waalikwa waliokuwa nje ya msikiti walikuwa wanateta jambo lililotokea,hakuna hata mmoja kati yao aliyejuwa kuwa Katrina amezirai kisa Issa.
*********
Kulikuwa kuna uwezekano mkubwa wa Issa kupoteza maisha yake endapo angekunywa chupa yenye maji mapema, kupokea simu ya Katrina ndiyo ilifanya mpaka wakati huo anapumua kwa shida na kutoa mapovu na kukoroma kama kondoo ndani ya gari akiomba msaada awaishwe hospitalini,hakuelewa watu aliokuwa nao ndani ya gari wanataka kuutoa uhai wake.
“Tunafanyaje Khan?”
Muhindi mmoja alimuuliza mwenzake baada ya kuona mambo yamebadilika.
“Tumuuwe humuhumu”
“Hapana,Khaila kapiga simu tumpeleke Aghakhan”
“Unadhani itakuwaje?”
“Nisikilize sasa,huyu tukimuulia humu itatuweka sehemu mbaya tutamuulia mulemule hospitali bila mtu yoyote yule kujua”
“Sasa akiamka si ataongea kila kitu”
“Kabla jua halijazama leo.Atakuwa marehemu.Kwanza muhesabie ni maiti tayari”
Wahindi hawa waliteta kwa lugha ya kihindi wakijadili watumie njia ya aina gani kumtowesha Issa duniani ingawa waliamini kuwa hatofika hospitalini kutokana na hali yake kuwa mbaya zaidi,mbali na hapo alishaanza kutoa mapovu mdomoni hiyo iliashiria kuwa Israel mtoa roho za watu yupo mita chache na muda wowote Issa angeaga dunia.
Dereva akapewa amri ageuze gari na kwenda hospitali ya Aghakhan na huko ndipo walipanga wamuulie Issa vizuri,Ilikuwa ni bahati nzuri kwa Issa na mbaya kwa wahindi hawa kwani barabara ilikuwa nyeupe kabisa hiyo ilichukuwa dakika chache sana kufika hospitalini,akashushwa kutoka kwenye gari na kupakiwa kwenye machela ambapo magwiji wa kucheza na miili ya binadamu walitokeza wakiwa na mtungi wa hewa ya Oxygen,wakamvalisha puani hali ya kutoa mapovu ndiyo iliwachanganya zaidi hiyo ilikuwa kama wanajaribu bahati ya kuokoa maisha ya kijana huyu mdogo kufa.Uwepo wa Issa hospitalini hapo na Katrina ulifanya madaktari kuhaha mno sababu walijua uhusiano wao na bosi,hivyo uzembe haukutakiwa ndiyo maana kila daktari alishughulika na alikuwa makini kuliko kawaida.Machela aliyolala Issa ilipitishwa mbele ya macho ya dokta Khaila,akaisogelea na kuona jinsi Issa alivyokuwa ana mapovu shingoni na mdomoni mwake,hiyo ilimfanya achanganyikiwe zaidi na ingetokea habari mbaya yoyote ile siku hiyo alijuwa kabisa Katrina asingekubali na yangeibuka matatizo mengine zaidi ya hayo.Bado hakuelewa imekuaje mpaka Issa akawa anatoa mapovu namna ile.Alikuwa katika Kitendawili kikubwa sana na hakuna mwingine ambaye angekitegua isipokuwa shemeji yake Khan,ndiyo maana alivyomuona alimuendea kwa kasi.
“Imekuaje?”
Bila salamu aliuliza huku akiwa anahema kwa jazba.
“Njoo tuongee pembeni”
“Shemeji imekuaje?Hakuna haja ya kuongea hili swala pembeni.Niambie nini kimetokea”
“Mimi sijui chochote,tulikuwa ndani ya gari vizuri tu.Nashangaa anasema tumbo linamuuma.Tukajua kawaida lakini hali yake ikazidi kuwa mbaya sana.Kufika pale Msikitini ndio akadondoka akaanza kutoa povu mdomoni”
Hayo yalikuwa maelezo ya Khan akiwa mkavu wala hacheki,ungemuangalia ungesema anaongea ukweli sababu aliongea huku akisikitika.Dokta khaila hakuwa ana kitu chochote kile cha kuuliza.
“Eh Mungu”
Akasema huku machozi yakimlenga.Macho yake yote yalikuwa mlangoni kwa daktari aliyekuwa chumba alicholazwa Katrina na mlango ulivyofunguliwa akapiga hatua kubwa mpaka kwa dokta.
“Vipi hali ya Katrina?Anaendeleaje?Tatizo nini Dokta?”
Dokta Khaila aliuliza maswali mengi mfululizo hiyo ikamfanya mpaka daktari ashindwe aanze kujibu kipi na amalize lipi.
“Ana hali nzuri,alipata tu mshtuko wa..”
“Naweza kumuona?”
Kabla ya daktari kumaliza Dokta Khaila akauliza kwa shauku.
“Ndio”
Sijui kama aliuliza kitu kingine zaidi,akasukuma mlango na kuingia mpaka ndani ambapo alimuona Katrina amelala juu ya kitanda machozi yanamtoka haongei kitu chochote kile,akamsogelea mpaka karibu kabisa!
“Katrina,unaendeleaje?”
Mama akauliza kwa sauti ya chini huku akidondosha chozi moja la uchungu.
“Naendelea vizuri,Issa yuko wapi?Nataka nikafunge ndoa”
“Issa yupo”
“Nataka kumuona”
Ombi hilo lilimfanya Dokta Khaila apate kitete,ni wazi kuwa hakuelewa hali ya Issa inaendeleaje tangu alivyoingizwa hospitalini.
“Atakuja usijali”
“Mamaaaa,nataka kumuonaa sasa hivi au niende mwenyewe?”
Haikushindikana kwa Katrina kuchomoa dripu kwenye mshipa wake wa damu na kuanza kuingia kila wodi akimsaka mpenzi wake ndiyo maana Dokta Khaila alimtuliza na kumwambia kuwa ataenda kumuita ingawa hakuelewa kama swala hilo litawezekana,alisema hivyo ili kumtia moyo na kumpa matumaini.
“Maaaama”
Katrina akaita kwa sauti,bado alikuwa dhaifu.Mama akageuka alikuwa ameukaribia mlango!
“Nahitaji kufunga ndoa hapahapa hospitali,mwite shekh nije kufunga ndoa na Issa.Nampenda,nahitaji kumuona”
Yalikuwa ni maneno makali na wakati huohuo ya kuuzunisha mno,Mama Katrina bila kujibu chochote alitoka nje na breki ya kwanza aliuendea ukuta na kuanza kumwaga machozi mfululizo,alilia kwa uchungu mpaka ngozi yake ikabadilika rangi na kuwa nyekundu.
Hakuelewa ni kwanini matukio ya ajabu yanamtokea sambamba namna hiyo.Dakika tano nzima alikuwa ukutani,akatoa kitambaa na kujifunika usoni ambapo aliendelea kulia tu.
“Dokta”
“Ye..s”
Akaitika kwa kwikwi baada ya kushtuliwa na daktari aliyetokea nyuma yake,kabla ya kugeuka akapangusa machozi yote.
“Pole sana”
“Nishapoa,Issa anaendeleaje?”
“Bado yupo ICU lakini hali yake sio nzuri sana”
“Tatizo ni nini?”
“Alikunywa kitu chenye sumu kali ya DDT”
“Whaaaat?”(Niniiiii)
Ulikuwa ni mshangao wa waziwazi.
“Ndio dokta na mbaya zaidi imesambaa kwa kiasi kikubwa sana mwilini.Tuombe Mungu”
Yeye mwenyewe alikuwa ana taaluma ya udaktari maneno hayo alijuwa yana maanisha nini,kupona kwa Issa ilikuwa ni asilimia kumi tu jambo ambalo hakutaka litokee kabisa sababu angemkosa Katrina kwani nayeye angejiua kama sio kupooza mwili mzima.
“Fanyeni juu chini”
“Tunaendelea kujitahidi”
“Sa..”
Kabla ya Mama Katrina kujibu,alikatishwa na machela kutoka chumba kinachofuata.Juu kulikuwa na mtu aliyefunikwa shuka la kijani.Moyo wake ukapiga paa na nguvu zikamuishia sababu alielewa nini maana yake!




Dokta Khaila alipata mshtuko wa ajabu sana na mapigo yake ya moyo yalikita kwa hofu iliyomtanda,fikra zake zilimtuma moja kwa moja kuwa aliyekuwa juu ya machela ni Issa ingawa hakutaka kulipitisha swala hilo moja kwa moja katika akili yake ndiyo maana alimuomba Mungu isiwe hivyo.Wasiwasi aliokuwa nao Dokta Khaila kujumlisha na macho yake alivyokuwa ameyatupa juu ya machela ilimfanya Dokta ajuwe nini tatizo la tajiri yake.
“Issa yupo chumba kinachofuata”
Hayo yalikuwa maneno ya dokta lakini Mama Katrina aliendelea kugandisha macho juu ya machela bado hakuamini kama amesikia vizuri ama dokta alitaka kumtia moyo.
“Chumba kipi?”
“Kinachofuata”
“Kule I.C.U?”
“Ndio”
“Mbona mara ya kwanza uliniambia yupo thieta?”
“Nilichanganya Mama,hata mimi nilichanganyikiwa”
Mama Katrina pamoja na daktari waliongozana mpaka chumba alicholazwa Issa ambacho kabla ya kuingia walichukua makoti ya rangi ya bluu,wakaacha viatu vyao nje na kuzama ndani.Dokta Khaila alihisi kulia sababu mdomo mzima wa Issa ulizungukwa na mashine na Issa hakujigusa wala hakujitingisha isipokuwa mashine ndizo zilikuwa zinapiga kelele kuashiria kuwa kuna uhai.
“Atapona?”
Dokta Khaila akahoji,alionekana kama mtu asiyekuwa na matumaini kabisa.
“Atapona ndio”
“Ulisema alikunywa sumu?”
“Ndio,DDT ni sumu kali sana hata hivyo tulijitahidi kwa kiasi cha kutosha mpaka hapa”
Issa alikuwa juu ya kitanda haelewi kitu chochote kinachoendelea ulimwenguni,kifupi alikuwa nusu mfu na uhai wake ulisaidiwa na mashine zinazomzunguka pamoja na dawa alizochomekewa puani na kwenye mishipa ya damu,hizo zilikuwa zinasaidia kuuwa sumu iliyokuwa tayari imesambaa mwilini mwake lakini vinginevyo angekuwa ahera.Dokta Khaila alikuwa I.C.U bado haamini tukio zima lililotokea siku hiyo,aliumia na hakuelewa ni kivipi Issa alikunywa sumu,taa nyekundu ikaanza kuwaka kichwani kwake kuashiria kuwa kuna jambo la hatari.
“Naomba Katrina asijuwe kuhusu hili jambo”
“Sawa Dokta”
Hilo lilikuwa pendekezo kutoka kwa Dokta Khaila kwani alijuwa nini maana yake endapo Katrina akibaini Issa ana hali mbaya sana.
Ndani ya chumba hiko maalum kwa ajili ya wagonjwa maututi kulikuwa na kioo kikubwa cheupe ambapo hata ukiwa kwa nje unaweza kuona kitu kinachoendelea ndani,alivyoangalia kwenye kioo akapungiwa mkono wa ishara kuwa atoke nje na dokta mwingine aliyefahamika kwa jina la Kajol,huyu pia alikuwa muhindi mwenzake.Taratibu akatoka mpaka nje.
“vipi?”
“Katrina anakuita”
“Anasemaje?”
“Sijui, kasema nikuite”
“Sawa”
Akili yake ikaanza kufanya kazi kwa haraka mno na kuanza kutafakari ni majibu gani ampe Katrina juu ya Issa sababu aliamini ndiyo maswali atakayoenda kukumbana nayo lakini kabla ya kuanza kufikiria,nyuma yake akatokea shemeji yake, Khan.
“Vipi hali ya mgonjwa?”
“Anaendelea vizuri tu”
Jibu hilo lilimfanya Khan ashtuke na aogope kupita kiasi kwani zilikuwa ni habari mbaya sana kwa upande wake sababu alitegemea Issa angekuwa amekufa tayari ama ana hali mbaya inayotisha ndiyo maana alitulia kidogo akitafakari,kuzinduka kwa Issa ingekuwa hatari kubwa sana kwake hivyo hakukuwa na njia nyingine yoyote zaidi ya kumziba mdomo kwa kumuuwa akiwa juu ya kitanda bila fahamu zake kumrudia,hilo aliapia angelifanya siku hiyohiyo.
“Atapona Subana Allah atasaidia”
“Inshallah”
“Inshallah”
Khan alijifanya kuonesha simanzi kubwa sana usoni lakini rohoni alikuwa chui mkali na siku zote moyo ni kiza kinene huwezi kujua yupi adui yako.Dokta akaachana naye na kuamua kuingia ndani ya chumba cha Katrina bila kujua kichwani mwa shemeji yake kuna mikakati ambayo ingegharimu mpango wote mzima wa matibabu ya Issa pamoja na Katrina.
“Mamaaa…Issa yuko waaapi?”
Katrina akahoji bila ya kukwepesha maneno,kuna dalili fulani fulani alianza kuzihisi ambazo hazikuwa nzuri.
“Unaendeleaje?”
“Mama nahitaji kumuona Issaa,yuko wapi kwani?”
“Amechomwa sindano ya Usingizi,amepumzika.Hautoweza kumuona sasa hivi”
“Nahitaji kumuona Mama,naombaaa.Nataka tufunge ndoa,leo ni siku yetu”
“Katrina pumzika”
“Hapana siweziii bila kumuona Issa”
Japokuwa walitumia sauti ya chini kuzungumza lakini sauti ya Katrina ilianza kupanda taratibu mwisho ikawa kali.Alichotaka yeye ni kumuona Issa mbele yake na wala sio mambo mengine kabisa na ndiyo maana akataka mpaka kuchomoa dripu mkononi.
“Katrina tulia,Issa amepumzika”
Mama nayeye akapandisha sauti lakini haikusaidia kumfanya Katrina apoe kwani aliinuka na kukaa kitako kitandani.
“Tulia Katrina”
Maelewano hayakuwepo tena kati yao hiyo ikafanya mpaka madaktari wengine waingie wodini kuangalia nini kinaendelea.
“Issa yuko wapi?Saida nambie alipo Issa niende”
Swali hilo lilitua kwa muuguzi aliyeitwa Saida na Katrina aliuliza kwa jazba huku akihema juu juu,ilibidi wote wamwangalie Dokta Khaila ili atoe ruksa.
“Dokta Khaila,inabidi Katrina ajuwe ukweli”
Mmoja wapo alishauri na kauli hiyo ilifanya mapigo ya moyo ya Katrina yapige kwa nguvu mno sababu kivyovyote vile aliamini kuna habari mbaya.
“Mama, Issa amekufa?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Katrina na alikuwa ana kila sababu ya kuuliza hivyo ingawa hakutaka kusikia jibu ‘NDIO ISSA AMEFARIKI’ sababu ingepelekea nayeye kujiua siku hiyohiyo.
“Hapana lakini ana hali mbaya sana”
“Naomba mnipeleke nikamuone”
“Pumzika kwanza”
“Siwzei kupumzika,naomba nikamuone Issa”
Kufuatia hapo hakuna kipingamizi kingine chochote kile kilichowekwa sababu walielewa fujo za aina gani zingetokea endapo wasingekubali matakwa ya Katrina,wakamshusha kitadani na kumtoa plasta kisha kuanza kutembea naye mpaka chumba cha wagonjwa mahututi yaani I.C.U ili akamuone Issa wake.
Taratibu zilikuwa zilezile kuvaa nguo maalum za kuingia chumba hiko kilichokuwa na utulivu wa hali ya juu sana,kilichosikika zilikuwa ni mashine za mapigo ya moyo.Kitendo cha Katrina kutupa macho juu ya kitanda alicholala Issa aliangua kilio na kumsogelea karibu,akalala juu yake.
“Issaaa amk..a mu..me wan..gu tukafu..nge ndoa”
“Katriinaa”
Mama akaita kwa nyuma na kumshika bega akitaka kumtoa lakini wapi.
“Iss…a amk..a mume wa..ngu..Amka.. kwanini wewe?Kwani..ni amk..a kumbuka aha..di yako ulisema hutonifa..nya nili..e amka Darling”
Katrina aliendelea kulia kwa kwikwi na kumfanya mpaka Mama yake aanze kumwaga machozi,ikawa kama wapo msibani.
“Amefa..nya nini?Madaktari walisema nin..i?”
“Alikunywa kitu chenye sumu”
“Sa.aa nga..api?”
“Leo asubuhi alivyokuwa anaenda msikitini”
“Na..ni kafanya hivi?”
“Bado hatujui”
Mpaka inafika saa kumi jioni Katrina alikuwa chumba alicholazwa Issa wala hakutaka kubanduka kwenda sehemu yoyote ile.
Japokuwa alisisitizwa aweke angalau kitu chochote mdomoni lakini hakuweza sababu akili yake yote ilikuwa kwa mgonjwa anayempenda kuliko kitu chochote kwa maana hiyo chakula kisingepita kabisa.Utata ulizuka kichwani mwa Katrina juu ya sumu iliyosemekana kumuweka kitandani akawa mahututi, bado haikumuingia akilini hata kidogo ni lazima kulikuwa na mtu mbaya sana nyuma ya jambo hilo,hayo ndiyo yalikuwa mawazo ya Katrina akiwa juu ya kochi peke yake amekaa,amechoka kupita kiasi.
************
Miguu ya Issa ilikuwa ikicheza kama kuku aliyekatwa kichwa,anahangaika kutafuta hewa, hiyo ilifanya Katrina akarupuke kutoka kitini kama sungusungu aliyepoteza kirungu,aliogopa kwa kiasi cha kutosha na kufanya apige kelele nyingi sana zikapenya mpaka nje,madaktari wakafungua mlango na kumvaa Issa.
“Katrina kaa pembeni”
Daktari mmoja wapo akatoa kauli hiyo huku akimsogelea Issa karibu kabisa,akaangalia mashine jinsi inavyopiga kelele zaidi.Mapigo ya moyo yalikuwa yanateremka.Haraka akatoka nje na kuwaita wenzake ambapo walifika na chupa ya dawa,wakaingiza sindano na kuvuta dawa ndani ya bomba.Wakati hayo yote yanatokea Katrina alikuwa akishuhudia kwa macho yake huku akiwa kama mtu aliyerukwa na akili.
“Tiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii”
Mashine ikatoa mlio mmoja tu na kufanya madaktari wote wasitishe zoezi zima la kumshughulikia Issa,walishaelewa nini maana yake.Katrina alielewa sababu hata yeye alikuwa ni daktari mashine kutoa mlio huo ilimaanisha kuwa mapigo ya moyo yamesimama,kifupi kila mtu aliganda na kikatolewa kipima moyo ili kuhakikisha kama ni kweli.
“He is gone”(Amefariki)Dokta akasema kwa kiingereza huku akitikisa kichwa kwani juhudi zao za kutaka kuokoa maisha ya Issa, zilidunda.
Ilikuwa ni kauli ya kutisha kupita kiasi na bado Katrina hakutaka kukubali moja kwa moja ndio maana akawa kama mtu aliyepalalaizi,mwili wake ukawa kama umepigwa sindano ya ganzi.Issa alikuwa juu ya kitanda amelala haongei chochote kile,ameshakufa.Hivyo ndivyo ilivyokuwa.
“Iss…a Iss…a”
Bado hakutaka kuamini kama Issa ametoweka duniani kwa staili hiyo tena siku ya harusi yake, ndio maana akasogea na kuanza kupiga kelele kama mwehu.
*******
Katrina alikurupuka kutoka kwenye sofa kama mtu aliyemwagiwa maji na kuangaza huku na kule ulikuwa tayari ni usiku,alikuwa ni kama mwenye mawenge na ilionekana alilala kwa masaa mengi kutokana na uchovu mwingi.Akili yake bado haikukaa sawa sawa,ndoto aliyoota kuwa Issa amefariki ilimtisha mno,alivyoangalia mbele yake alimuona Issa anatingisha miguu na pembeni alikuwa amesimama mjomba wake Khan,amempa mgongo kivyovyote vile kulikuwa kuna kitu kibaya kinaendelea moyo wake ukapiga kwa nguvu,akasimama.Hata hivyo alikuwa sahihi sababu Khan alikuwa amebana mrija unaopitisha hewa ya oksijeni ndani ya mapafu ya Issa ili amuuwe,aliamini njia hiyo ndiyo sahihi na angefanya haraka kwani alimuona Katrina amelala usingizi kipindi anaingia.Wakati anaendelea kuubinya waya wa hewa,alishtuka baada ya kusikia jina lake linaitwa.
“Mjomba Khan”
Katrina aliropoka sababu alisogea karibu na kuona tukio zima, moyo wake ulimuuma hapohapo akaanza kupiga kelele kwa sauti kubwa akiomba msaada.
“Doktaaaa doktaaaaa”
Katrina akapiga ukelele, hiyo ilimfanya Khan atimue mbio na kuparamia mlango akijaribu kukimbia.



Kitu kilichotokea ilikuwa vigumu kuamini hata kidogo,ndiyo maana alidhani yupo ndotoni ingawa alitoka kwenye njozi muda mfupi uliopita.Khan alihisi kuchanganyikiwa mno,alitoa mbio zisizokuwa za kawaida sababu aliamini nini maana yake endapo angeanguka kwenye mikono ya sheria,ndiyo maana alipangua pangua manesi na madaktari kwenye korido, kila mtu aliyemuona alimshangaa wengine walidhani wenda ni mgonjwa alipandwa na Malaria kichwani.Katrina alibaki njia panda hakuelewa ni kitu gani akifanye zaidi ya kupiga kelele kwa sauti kubwa,madaktari wakasogea mbio mbio na kuzama ndani.Hali waliyomkuta nayo Issa hata wao waliogopa kupita kiasi,bila kuuliza wakaweka kila kitu na kumchoma sindano lakini bado miguu ya Issa iliendelea kujitingisha kama mtu anayekata roho hiyo ilimuogopesha Katrina zaidi na kumfanya aanze kuwashika madaktari makoti.
“Mtoe nje”
Daktari mmoja alishauri,akimaanisha Katrina atolewe nje ili kazi yao iendelee bila bugudha yoyote ile.
“Katrina,twende nje tuache tufanye kazi yetu”
Hayo ndiyo maamuzi waliyochukuwa madaktari,Katrina akatolewa nje lakini haikuwa kazi rahisi kumtuliza na kilichomuumiza moyo na kumkumbuka Mungu ni kuhusu ndoto aliyoota muda mfupi uliopita kuwa anapewa habari kwamba Issa amefariki dunia jambo ambalo hakutaka litokee ndiyo maana akawa anateta na Mungu wake aliye juu Mbinguni.
“Nini kimetokea?”
Mama yake Mzazi ndiye aliyetokeza nyuma yake na kumshika bega, akitaka kujua nini kilisababisha mpaka Issa achezeshe miguu namna hiyo,Kwa kwikwi na kilio Katrina akaanza kumwambia kila kilichotokea.
“Khan?”
“Ndi..o Ma..ma”
“Yuko wapi?”
“Amekimbia s..ij..ui al...ipo”
Mama Katrina alikabwa na hasira kohoni, hakutegemea kama Shemeji yake angetaka kufanya jambo kama hilo la kinyama ndiyo maana akakimbia moja kwa moja katika uongozi wa Ulinzi wa hospitali hiyo na kutoa taarifa mtu huyo akamatwe mara moja,hospitali yake ilikuwa ya kisasa yenye kamera kila kona.Hivyo haikuwa kazi ngumu kumsaka wapi alipo.
“Yupo parking yard,ndio anawasha gari anataka kuondoka”
Huyu alikuwa mlinzi kutoka katika kampuni ya KK security alikuwa ni mtanzania na ndiye aliyeonekana kuwa kiongozi wao,Khan alionekana kwenye kioo kikubwa cha televisheni akiwa anaingia ndani ya gari.Bila kupoteza wakati kupitia redio upepo ikapigwa getini kuwa gari yake isiruhusiwe kutoka nje na awekwe chini ya ulinzi.
Maaskari wa kampuni hiyo walikuwa makini sana na kazi yao kwani kitendo cha Khan kufika getini kundi la walinzi liliibuka mbele ya gari lake na kumuweka chini ya ulinzi hapohapo,akawa hana ujanja tena akajuwa tayari amekwisha na anaenda kunyea ndoo gerezani kwa kosa la kujaribu kuuwa.Dokta Khaila alivyofika akamtizama kwa jicho la hasira kali na hakuwa na cha msalia Mtume, akapiga simu polisi ili waje kumchukuwa.
“Shemeji unafanya makosa sana.Issa ni najisi”
Khan alikuwa akiongea akiwa mikononi mwa Polisi anaingizwa ndani ya gari na tukio hilo lilijaza baadhi ya watu sababu askari waliingia kwa mkwara mzito na mbwembwe nyingi.
“Ingia ndani ya gari.Muuwaji wewe, muhindi koko”
Askari mmoja akasema,wakamuingiza Khan ndani ya gofu la polisi.Ambapo huko hawakuwa na kitu kingine zaidi ya kumminya,ndani ya masaa mawili akataja wote waliohusika kwenye mpango huo wa kinyama wakitaka kumuuwa Issa,Polisi wakaingia mzigoni kumzoa mmoja baada ya mwingine na kuwatupa lupango.
***** *****
Hali ya Issa ilianza kuwa mbaya mno,hiyo ilifanya madaktari wazidi kuchanganyikiwa kupita kiasi na ilimchukuwa muda mrefu sana Katrina kutulia,sababu machozi yalimkauka kabisa.Mpaka inafika usiku saa tatu hakukuwa na dalili yoyote ile ya matumaini kabisa ingawa walimfanyia CPR yaani ‘Cardioo Pulmonary Susection’ hapo walitaka kumpa mgonjwa pumzi kwa maana hiyo walikuwa wanakikandamiza kifua chake lakini wapi.
Kufikia hatua hiyo walijuwa kivyovyote vile ni lazima Issa angeaga dunia ndiyo maana madaktari walikuwa tayari kupokea msiba siku yoyote kuanzia siku hiyo lakini hawakutaka kuwa wawazi kabisa.
“Ma…ma nata..ka kufunga ndo..a na Issa akiwa hospitalini..Hata Akifa…”
Katrina alishindwa kumalizia maneno aliyokuwa anataka kuzungumza akiwa nje na Mama yake,alihisi uchungu ajabu.Wakati mwingine alijiona ana mkosi ama gundu katika ulimwengu wa mapenzi.Baadhi ya ndugu jamaa na marafiki pamoja na wageni ambao walialikwa kwenye harusi,walianza kupiga simu wakitaka kujua nini kimetokea lakini Katrina hakuweza kuongea chochote sababu ya maumviu aliyokuwa nayo,kwake ulikuwa ni kama msiba mkubwa sana.
“Ma..ma Issa akifa..a nami..mi najiua sito…weza kule..a huyu mto..to mwenyewe”
Katrina aliongea vitu viwili vilivyomshangaza Mama yake kwa wakati mmoja.Alishindwa kuelewa kama ni kweli Katrina ana ujauzito au ameropoka tu.Licha ya hayo alizungumza maneno mazito kutamkwa,kufa kwa Katrina mtoto wake wa pekee kungefanya maisha ya Dokta Khaila yayumbe.
“Katrina una mimba?”
Mama akauliza kwa mshangao,hakuwa na habari tena na Issa!
“Ndi..o Mama”
“Mbona hukuniambia?”
“Ma..ma Issa wangu nata..ka nifunge naye ndoa”
“Katrina,Allah ataweka mkono wake!Issa atapona”
“Ma..ma nimeota ndoto.Atakufa”
“Usiwe unaweka kichwani ndoto mwanangu,Issa atapona”
Katrina alihisi kufarijika lakini bado ndoto aliyoota ilimfanya akose raha na Amani kabisa.Kila sekunde ilivyozidi kwenda mbele ndipo hali ya Issa ilizidi kuwa mbaya zaidi ikafika kipindi mwili wake ukawa unacheza kama mtu mwenye degedege ama kifafa hiyo iliwafanya madaktari wazidi kuhaha zaidi ndani ya chumba cha wagonjwa mahututi alicholazwa Issa.
“Sidhani kama atapona,sumu imeingia pabaya sana.Lakini ni nani aliyechomoa waya wa Oxygen?”
“Yule muhindi shemeji yake na bosi”
“Ndio kafanya mambo yanakuwa magumu kidogo.Hapa labda muujiza utokee”
Ilikuwa ni wazi kwamba hata madaktari waliobobea walinawa mikono na shughuli hiyo ilionekana kuwa nzito mno,ndiyo maana walijigawa na kuweka kikao kidogo cha kuteta juu ya kitu gani wakifanye.
“Mchome Hydrocortisone.Ili ipunguze tena makali ya sumu”
“HiYo tayari”
“Mchome tena”
“Sawa”
Hicho ndicho kitu kilichofanyika dakika hiyohiyo na kazi ya dawa hiyo aina ya Hydrocortisone ilikuwa ni kupunguza sumu mwilini.Na hiyo ndiyo iliyomsaidia kwa mara ya kwanza sababu ilikuwa ni tofauti alivyopelekwa hospitali hapo awali kwani alikuwa wa njano mwili mzima.
“Hii sumu ya DDT ni kali sana.Huyu mgonjwa ana bahati ni kama muujiza”
Madaktari bado walishangazwa na mgonjwa huyo ambaye mpaka wakati huo alikuwa anapumua, ilikuwa ni tofauti kabisa kwa wagonjwa wengine ambao waliwahi kufikishwa hospitalini hapo wakiwa wamekunywa sumu hiyo kali ya DDT poison iliyokuwa na uwezo wa kumuondoa kiumbe hai ndani ya dakika tano tu.
Dokta Khaila aliwasumbua mno madaktari kwa kiasi cha kutosha ndiyo maana aliingia na kutoka ndani ya chumba hicho,hata yeye hali ya Issa iliibua viulizo vingi kichwani kwake na hakuwa mwenye matumaini tena lakini alivyotoka nje alibadili uso na kuweka tabasamu bandia ili kumfariji binti yake, Katrina!
“Anaendelea vizuri sasa hivi,wamemchoma tena Hydrocortisone”
“Ametulia?”
“Ndio Katrina”
“Naweza kumuona?”
“Hapana.Mwache apumzike kidogo”
“Mama unanidanganya”
“Katrina,Issa anaendelea vizuri”
Japokuwa alikuwa mwenye wasiwasi lakini alijipa moyo kuwa Issa atapona sababu yote alimuachia Mungu wake aliye juu Mbinguni,hiyo ilifanya wasubiri juu ya benchi.
“Mjomba Khan amekamatwa?”
Katrina akahoji baada ya kukaa kwa muda mrefu bila kuongea chochote.
“Ndio,kumbe hata Raul anahusika vilevile”
“Bam kubwa Raul?”
“Wote hao,walipanga njama wakamuwekea Issa sumu kwenye maji ya Kunywa ili afe”
Kitu hicho kilimuuma sana Katrina,haikuwezekana hata kidogo Baba yake mkubwa aliyeitwa Raul kutenda jambo kama hilo sababu alimuheshimu na walikuwa marafiki wakubwa sana.
“Kwanini lakini?Nampenda Issa.Nampenda,Mungu amenipa yeye.Kwanini wanataka kufanya hivi?Mama waambie ndugu zako”
Katika maneno yake hakukuwa na punje ya masihara hata kidogo na alisema hayo kutoka ndani ya shina la mtima wake.Mpaka inafika saa tisa za usiku Katrina hakutoa makalio yake juu ya benchi ingawa mbu walimng’ata lakini hiyo kwake haikuwa kitu kabisa,Saa kumi kasoro ilivyofika waliona chumba alicholazwa Issa kinafunguliwa mlango na madaktari wawili wanatoka.
Mbaya zaidi walikuwa wanaonesha sura za huzuni na ilionekana kama wanajadili kitu fulani huku wanamtizama Katrina na Mama yake,picha hiyo haikuwa nzuri kwa Katrina hata kidogo, kuna kitu alijifunza ndiyo maana akasimama wima na kuwaendea kwa haraka.
“Issa anaendeleaje?”
Akauliza huku akiwatizama machoni,hiyo iliwafanya madaktari wapate kigugumizi cha ghafla.
“Issa ame…Ame……”
***********
Maisha ya Deo Karekezi yalibadilika ghafla,kufumba na kufumbua alikuwa amepoteza kila kitu kuanzia mali mpaka magari yote licha ya yote kampuni yake ilifilisiwa, hisa zake zote ziliuzwa ili deni analodaiwa na Katrina lilipwe mbali na kufanyiwa unyama huo alihukumiwa kifungo cha miaka kumi na tano gerezani jambo ambalo hakuwahi kuliota hata siku moja,Maisha ya jela kwake yalikuwa kama Jehanam!Milo mizuri aliyokuwa anakula, viwanja alivyokuwa anatembea, magari aliyokuwa anaendesha havikuwepo tena.Aliwakumbuka sana marafiki zake na starehe zote.Alivyomkumbuka Mwanaye Abraham ndiyo aliumia zaidi,miaka kumi na tano ilikuwa mingi sana kwake.Ingawa alijitahidi kuzoea lakini wapi,kila siku alionekana kuwa mnyonge na alijitenga na wafungwa wenzake sababu hakutaka kujichanganya nao,kwa siku walikuwa wanakula mlo mmoja tena chakula wakati mwingine hakikuiva vizuri na kilijaa wadudu wengi.
Kama siku yakipikwa maharage basi hujazwa maji mengi na ugali unakuwa na mabuja.Siku ya nyama kwa wafungwa ilikuwa ni sherehe kubwa sana tena waliifananisha na sikukuu ya Idd ama Chrissmas ndiyo maana huwa wanafanya fujo wakigombea nyama.Hiyo ilimuumiza sana Deo sababu hakuweza kugombania hata kidogo,kila siku alikuwa mtu wa kulia na kusikitika.Kwake masaa yalikuwa hayaendi kabisa na mpaka unafika mwezi mmoja hakuamini kama yupo gerezani.
“Deo Karekezi”
Sauti ya askari Jela ndiyo iliyomshtua akiwa kwenye kona ya pembe peke yake.Akasimama na kutembea taratibu mpaka kwenye nondo.
“Ndio wewe?”
“Ndio afande”
“Njoo huku”
Askari Magereza akafungua kufuli,Deo akapigwa pingu na kuanza kuongozana naye.
“Ulikuwa hujui kwamba leo ni visiting day?”
“Hapana mimi sijui”
“Ndugu yako amekuja kukuona”
Waliongozana na askari Jela mpaka sehemu maalum ya watu wanaokuja kuona ndugu zao waliofungwa na wakati mwingine kuwaletea chakula,Deo alitaka kumuona mtu aliyekuja kumtembelea.
“Mtuiiiii”
Deo ndiye aliyeita.
Mtui alivyogeuka alijisikia uchungu ajabu na kushindwa kujizuia kulia,Deo alitia huruma na mwili wake ulipungua uzito mbali na hapo ulijaa ukurutu.Hakuwa Deo yule wa zamani mtanashati, ndiyo maana Mtui aliingiwa na huruma akaanza kulia kama mtoto mdogo,akatoa kitambaa na kujifunika usoni.Tukio hilo lilimfanya na Deo ashindwe kuvumilia japokuwa hakuelewa ni kwanini Mtui analia,akajikuta anaungana naye.
“Deo pole sana ndugu yangu”
Mtui akasema huku akifuta machozi maana alilia kama mwanamke,ulikuwa ni uchungu ambao hakuwahi kuusikia,aliamini kabisa Deo hakustahili mateso kama hayo.
“Ahsante,nishapoa”
“Ndio Maisha.Katika maisha uwe tayari na jambo lolote lile.Hizi ni changamoto,kila jambo lina makusudi yake hapa duniani”
“Ahsante Mtui”
“Nimekuletea chakula hiki,kuna kuku hapa na nyama nyama za kuchoma na mishkaki”
Deo alivuta mfuko bila kuuliza akaanza kula,akapewa na maji makubwa ya Kilimanjaro na baada ya hapo wakaanza kuzungumza tena.
“Mtui naomba kitu kimoja unisaidie”
“Kitu gani?”
“Marietha anajua nipo hapa?”
“Hapana hajui na wala sijawahi kuonana naye”
“Kabla sijafa,naomba nimuone mwanangu Abraham”
“Nani kakwambia utakufa Deo?”
“Nina maana yangu kukwambia hivyo.Kama ikiwezekana naomba nimuone na Marietha kwa mara ya mwisho”
Katika maneno aliyoongea Deo alimaanisha sababu ni kweli,alitaka kujiua ili aondokane na mateso yanayomkabili duniani.



Gerezani, kwake ilikuwa sawa na Jehanam ndogo ndiyo maana alifikiria kujifunga kitanzi na kujiua aondokane na taabu na mateso yanayomkabili,kabla ya kufanya tukio hilo la kujiua alitaka kumuona mwanaye Abraham.Ngozi ya mwili wake ilibadilika na alionekana mtu aliyechoka mno!
“Deo”
Mtui akaita huku akimtizama Deo kwa masikitiko makubwa sana,moyo ulimuuma ajabu.
“Naam”
“Mimi naona Abraham asijue kama wewe upo hapa”
“Inabidi ajue,Mtui naomba mwezi ujao uje na Marietha.Hakikisha hilo linatokea”
“Nitajitahidi”
Waliongea vitu chungu mzima na Mtui alijaribu kumfariji swaiba wake,akimwambia kuwa siku hazigandi kila kitu kitaenda sawa kwani miaka kumi na mitano ni michache sana,hivyo ndivyo ilivyokuwa.Muda ulivyofika wakaagana na Mtui akaondoka zake huku kichwani akiwa ana kazi ya kumsaka Marietha kwa wudi na uvumba ili mradi ajuwe anaishi wapi.
Harakati na mipango ya kumsaka Marietha ilianza siku iliyofuata ambapo alienda Kimara kumuulizia kwa mara nyingine ambapo alipata jirani mmoja aliyemuelekeza kwa binti wa Kilokole aliyeitwa Tujaely Mnzava.
“Mbezi kule ndiyo yupo kwa sasa hivi”
“Mbezi sehemu gani?”
“Mbezi ya chini.Unalijua daraja la malesela?”
“Ndio,Si kama Mikocheni huku kwa chini?”
“Ndio,sasa ukifika pale.Kuna ile supamarket pale darajani.Hapohapo muulizie Mnzava Tujaely,ni msichana mmoja hivi ana macho makubwa ya duara mweupe.Ukimpata huyo basi umempata Marietha”
Hayo yalikuwa maelekezo ya Jirani ambaye aliwajuwa Deo na Marietha zaidi ya miaka sita na matatizo yote waliyopata aliyatambua pia,alisikitika lakini hakuwa na jinsi ya kufanya.Habari hizo zilikuwa njema sana kwa Mtui akaingia ndani ya gari na safari ya kwenda Mikocheni kuanza ambapo alichukua barabara ya Coca cola na kuingia Mikocheni B akaibuka Mlalakuwa huko alinyoosha moja kwa moja,akakumbana na round about na kunyoosha.
“Daraja la Malesela,Daraja la Maresela”
Alikuwa ni kama anaimba huku akiangalia huku na kule sababu aliamini anakaribia kulifikia.
Haikuwa mbali sana na alipokuwa sababu zilibaki mita chache,alivyoliona macho yake akayageuza pembeni ambapo aliona supamarket kubwa kiasi,hapohapo akapunguza mwendokasi na kuweka gari kando,akashuka na kuingia ndani.
“Karibu”
Sauti hiyo ilisikika kutoka kona ya mwisho kabisa,msichana aliyemuona alijaribu kumfananisha na maelekezo aliyopewa mwanzoni sababu msichana huyo alishahabiana kidogo na maelezo aliyopewa.
“Ahsante,samahani binti…..”
“Bila samahani”
“Namuulizia.Mnzava Tujaely”
“Wewe ukimuona utamfahamu?”
Akajibu kwa swali.
“Hapana lakini nimeelekezwa hapa,nina shida naye sana”
“Yupo njiani anakuja nadhani”
“Ahsante nitamsubiri”
“Okay”
Hazikupita hata dakika tano mlango ukasukumizwa akaingia msichana mnene kiasi,mwenye macho makubwa Mtui alivyomuona tu akajuwa ndiye yeye anayemtafuta lakini hakutaka kukurupuka moja kwa moja,mpaka alivyomshuhudia amekaa juu ya kiti karibu kabisa na binti aliyemkuta mara ya kwanza.
“Ancooo”
Mtui akaitwa na kusimama akatembea mpaka sehemu maalum kwenye malipo baada ya kufanya manunuzi ya supamarket.
“Mtu uliyekuwa unamtafuta ndio huyu hapa”
Tujaely aliganda kidogo na kumuangalia Mtui kwa kitambo, sura yake haikuwa ngeni hata kidogo,akajaribu kukusanya kumbukumbu zake kichwani.
“Habari yako dada”
Mtui akawa wa kwanza kutupa salamu kabla ya Tujaely kutafakari na kupata jibu la uhakika.
“Salama,samahani sijui nakufananisha.Kuna sehemu nilishawahi kukuona”
“Hata mimi sura yako sio ngeni kabisa”
“Eti eeeh?”
“Ndio”
“Nimepewa ujumbe hapa kuwa unanisubiri”
“Ni kweli mimi naitwa Mtui,ni rafiki mkubwa wa Deo ala…”
“Basi… basi… basi…nishakukumbuka.Tulionana kwa Deo siku ile ya vurugu ukawa umemshika Deo kwa nyuma”
Tujaely akafunguka jinsi alivyokutana na Mtui,kumbukumbu zikawa zimemjia hapohapo, akapata picha baada ya kutajiwa jina la Deo!
“Namimi nimekukumbuka”
“Deo mzima lakini?”
Swali hilo lilimfanya Mtui amwangalie Tujaely machoni sababu ilionekana hajui lolote,hakuelewa kabisa kuwa Deo yupo gerezani amehukumiwa kifungo cha miaka kumi na mitano.
“Ndio mzima.Nahitaji kumuona Marietha,yuko wapi siku hizi?”
Tujaely nayeye akatafakari kidogo hakuelewa atoe jibu gani sababu hata yeye hakujuwa ni wapi alipo,mbali na hapo alishamfukuza kwake wiki moja nyuma iliyopita.
“Marietha,alikuwa anaishi kwangu pale muda Fulani lakini akaondoka”
“Akaenda wapi?”
“Hakuniaga”
Tujaely hakutaka kufanya mlolongo uwe mrefu na wala hakuwa tayari kuongea mkasa uliotokea kati yake na Marietha,ukweli ni kwamba alimfukuza bila hata kutaka kumsikiliza alijisikia ni mkosaji na alijuta kufanya kitu kama hicho.
“Namba zake za simu?”
“Hakuwa na simu”
“Namtafuta sana,nina shida naye kubwa mno”
Huyu alimficha Deo alipo yule alidanganya Mazingira yaliyopelekea mpaka Marietha akaondoka kwake.

Kazi ya Mtui isingekamilika bila kumtia Marietha machoni ili ampeleke kwa Deo huko gerezani, hilo lisingewezekana bila kuelezwa alipo ndiyo maana akajaribu kumuuliza hata kwa marafiki zake wengine.
“Chukuwa hii namba,inawezekana yupo kwa huyu dada anaitwa Upendo John.Mtafute huko”
“Sawa ahsante”
Ilikuwa ni asubuhi ya saa nne na hapohapo Mtui akaanza kazi ya kumsaka Marietha sehemu moja mpaka nyingine,alivyompata Upendo John habari ilikuwa ile ile kuwa Marietha hakuwepo.Ilibidi apewe tena namba nyingine,akawasha gari mpaka Kigamboni Mjimwema huko napo mambo yalikuwa yaleyale,hakukata tamaa akaelekezwa mpaka Mbagala Mkulanga lakini hakuambulia chochote,mpaka inafika usiku wa saa mbili hakuwa ana dalili yoyote ile ya kumpata Marietha,alikuwa hoi bin taaban.
Mpaka inafika wiki moja alifanikiwa kumuulizia kila mahali alipoamini kuwa angempata lakini wapi,aliambulia patupu.Ulivyotimu mwezi mmoja baadaye na ilivyofika siku ya kuwaona wafungwa, kama kawaida Mtui alienda Gerezani kumuona swaiba wake Deo ili kumwambia kila kilichotokea.
“Kwahiyo umemkosa?”
“Ndio Deo,nimezunguka sana kumtafuta”
“Atakuwa Lushoto tu,hawezi kwenda popote pale”
“Lushoto? Tanga?”
“Ndio,yupo Tanga kwao”
“Nielekeze”
Maelekezo yalitolewa hapohapo,Mtui akawa ameshika kalamu na karatasi ili kuandika vituo vya kufika kwa Marietha.
“Nitajitahidi niende kumuona”
“Ahsante sana Mtui,hakika wewe ni ndugu yangu.Sina cha kukulipa lakini Mungu atakuongezea”
“No Deo huna haja ya kunishukuru kiasi hicho.Hii ni Dunia na matatizo haya tumeumbiwa sisi binadamu haya ni mambo ya kawaida sana kwa binadamu yoyote yule.Na waliofungwa vifungo vya maisha wafanyeje?Kesho kutwa tu hapo utatoka”
Mtui alimfariji rafiki yake na baada ya hapo wakaendelea kuongea vitu vingi sana,ilivyofika jioni wakaachana na alimuhakikishia Deo kuwa wakati mwingine angeenda na Marietha.
*******
Hatimaye Marietha aliingia mkoani Tanga kijiji cha Lushoto saa kumi ya jioni akiwa na watoto wake wawili amewashika mikononi,alikuwa hoi amechoka sana kutokana na safari kuwa ndefu kwake.Uchovu wake pia ulichangiwa na msongo wa mawazo pamoja na watoto kumtesa njiani,mbali na hapo alimshukuru Mungu kufika salama salmin,kwa mbali aliona nyumba aliyokuwa anaishi zamani, nje kulikuwa na akina Mama wanapepeta mchele,alitabasamu sababu aliwafahamu.
“Jamani Mariethaaaaa yule”
Mama mmoja aliacha ungo wa mchele na kusimama wima hiyo ilifanya wanawake wote wageuke,Marietha alirukiwa na walimlaki kwa furaha.
“Karibu Mama”
Lakini badala ya Marietha kufurahi baada ya kuwaona ndugu zake yeye alianza kulia machozi.
Alikumbuka vitu vingi sana nyuma,kwanza Mama yake mzazi aliyefariki kingine ni jinsi alivyopokelewa kwa shangwe nyumbani kwao,hakuamini!Kila mtu alimchangamkia na kumpokea watoto.
“Karibu Marietha,unalia nini?”
Mmoja wao aliuliza lakini Marietha aliendelea,akakaa chini kitako na kendelea kulia kwa kwikwi.
“Jamani Marietha una nini?Kuna nini?Kuna msiba?”
Alizidi kunyeshewa mvua ya maswali lakini ilikosa majibu kwani kohoni alibanwa na kwikwi kali mno,alitamani kuongea lakini alishindwa.
“De…o Deo ame….”
“Deo amefariki?Uwiiiiiiiiiii”
Mama mmoja kabla ya kusikiliza vizuri akaunganisha anachojua yeye,wanawake wote wakaanza kuangua vilio huku wakimtaja Deo.
“Deo jamaaaniiiii….Mungu weeee kwaniini umekweeenda?”
Sauti za vilio zilianza kusikika,Marietha alivyosikia hivyo akajikakamua na kusimama ili kuzuia kelele.
“Hapana Mama Mdogo,Deo ha..jafa”
“Hajafaaa!?”
“Ndioo”
“Kafanya nini?”
Wote wakakaa chini na kumsikiliza Marietha kile anachotaka kusema,ilibidi aongee ukweli kila kitu kilichotokea katika maisha yake tangu mara ya mwisho alivyochukuliwa baada ya msiba wa Mama yake kuisha na mambo yalivyoenda.
Kila kitu alikiweka wazi, hakutaka kabisa kukaa na kitu chochote kile kifuani mwake,akahadithia unyama aliofanyiwa na Amadour nchini Ufaransa na kumpata mtoto wa kizungu.Hakumaliza kwa kusema hayo aliongea na jinsi alivyofukuzwa na mumewe Deo na maisha aliyokuwa anaishi ya kutangatanga mitaani kama hana ndugu.Alivyohitimisha kusimulia mkasa huo wamama wote walikuwa wanalengwa na machozi.
“Pole sana Marietha”
Wakamkumbatia na kuanzia siku hiyo Marietha alipewa matunzo mazuri na ndugu zake,alikula vizuri na watoto wake walilelewa kwa uangalifu,alifarijika sana na hiyo ikafanya mpaka mwili wake unawili.
Siku hiyo akiwa nje mida ya mchana baada ya kama mwezi mmoja na nusu kupita aliona gari limepaki nje ya nyumba yao,Kwa mara ya kwanza alidhani ni Deo sababu gari zilifanana fanana,akakunja sura akaweka vyombo vizuri na kutaka kuingia ndani.
“Marietha”
Sauti hiyo ilimshtua,akageuka nyuma.Mapigo ya moyo ya Marietha yakapiga paaa!


ILIPOISHIA.
Alivyohitimisha kusimulia mkasa huo wamama wote walikuwa wanalengwa na machozi.
“Pole sana Marietha”
Wakamkumbatia na kuanzia siku hiyo Marietha alipewa matunzo mazuri na ndugu zake,alikula vizuri na watoto wake walilelewa vizuri,alifarijika sana na hiyo ikafanya mpaka mwili wake unawili.
Siku hiyo akiwa nje mida ya mchana baada ya kama mwezi mmoja na nusu kupita aliona gari limepaki nje ya nyumba yao,Kwa mara ya kwanza alidhani ni Deo sababu gari zilifanana fanana,akakunja sura akaweka vyombo vizuri na kutaka kuingia ndani.
“Marietha”
SONGA NAYO.

Mtui aliingia mkoani Tanga,Wilayani Lushoto saa kumi ya jioni na gari yake aliyoiamini aina ya Landcruiser Vx.
Kutokana na kupotea potea njia kila wakati ilifanya safari hiyo iwe ndefu kwake lakini alichoshukuru alifika salama na kitendo cha kuweka gari nje ya nyumba, alimuona mwanamke ambaye alifanya afunge safari yake kutoka mkoani Dar es salaam.Mapigo yake ya moyo yakabadili kasi na alijihisi kufanikiwa mno kwani kazi aliyotumwa na Deo ingekamilika wakati huohuo,alizima gari na kushuka ambapo aliita jina ‘Marietha’Wakatizamana kwa kitambo kidogo lakini Marietha hakuonesha uchangamfu hata kidogo sababu alijuwa nini Mtui alifuata.
“Habari za siku nyingi?”
Mtui akasalimia tena huku akisogea karibu na kutoa mkono wake ili wasahabiane lakini Marietha alitafakari kidogo bila kuutoa mkono wake kama kukubali salamu,alibaki akimuangalia Mtui machoni bila kusema chochote,vitu vingi sana vilipita ndani ya halmashauri ya kichwa chake na hakuja mwingine kichwani mwake bali ni mumewe Deo Karekezi na manyanyaso yote aliyopitia nyuma ya kuteswa kwa kiasi cha kutosha.
“Shemeji naomba tuzungumze kitu.Tuweke tofauti zetu kando”
“Tofauti gani?”
“Kuna mambo nataka kuzungumza nawewe ni muhimu”
“Siwezi”
Marietha alijibu na alimaanisha akatembea mpaka mlangoni na kunyonga kitasa ili azame ndani.
“Deo amefungwa,yupo gerezani”
Kauli hiyo ilimfanya Marietha asimame na kuganda,hakuelewa kama amesikia vibaya ama masikio yake yana uchafu wakati mwingine alidhani wenda Mtui anamtania ili anunue huruma yake hiyo ilifanya mpaka miguu yake ikakosa nguvu ya kupiga hatua nyingine mbele ili aingie ndani.
“Na anahitaji kuongea nawewe.Ni muhimu sana”
Mtui alizidi kuropoka na kusisitiza jambo analotaka kulisema,kwa kusema hivyo aliamini kwamba angeugusa mtima wa Marietha na hilo lilifanikiwa sababu Marietha aligeuka nyuma akitaka kujua alichosikia ni kitu halisi au Mtui anatingisha kiberiti.
“Deo amefungwa?”
Akauliza.
“Ndio”
“Kwanini?”
“Ni hadithi ndefu kidogo lakini kifupi anahitaji kukuona”
“Kuniona mimi?Hapana siwezi”
“Marietha tafadhali,nimefunga safari kutoka Dar.Mimi huku sipajui nimeelekezwa na Deo.Isitoshe mimi nawewe tunaheshimiana”
“Amejuaje kuwa nipo huku kama sio unafki”
“Kwa kweli sijui lakini nilikutafuta kila kona ya jiji.Marietha mimi nawewe tunaheshimiana na unaelewa hilo”
“Ndio naelewa”
“Basi naomba unisikilize”
“Siwezi shemeji na….”
Alikatishwa na Mama yake mdogo aliyeitwa Chiku kutokea ndani ya nyumba,ilielekea malumbano na sauti ya Mtui ndiyo iliyomtoa ndani ya nyumba ndiyo maana alitoka nje akitaka kumjua ni nani anayezungumza na Marietha.
“Habari yako anco”
Akatoa salamu.
“Nzuri tu,za kushinda?”
“Salama…Marietha mkaribishe mgeni ndani basi”
Hapo hakukuwa na kipingamizi kingine zaidi ya Mtui kukaribishwa ndani ambapo aliwasalimia wote aliowakuta,alivyotaka kuongea kilichomleta alisita sababu ya umati wa watu.
“Marietha”
“Abee”
“Tunaweza kuongea mimi nawewe kidogo pembeni”
“Hapana ongea tu hapahapa”
“Mamaaaaaaa”
Abraham ndiye aliyetokeza katikati ya Kordo akiwa anatembea mpaka kwa Mama yake,akamkumbatia.Moyo wa Mtui uliuma ajabu,alimuonea sana huruma mtoto huyu mdogo ambaye baba yake yupo gerezani.Abraham hakujua lolote sababu alikuwa yu mdogo sana,tabasamu lake lilikuwa furaha kwa Mama yake,Marietha.
“Nenda ndani Abraham”
“Taka cheza”
“Mbona hujamuamkia Anco”
“Chikamooooo”
“Marahaba hujambo Abraham”
Mtui akaitikia.
“Chijambooo.Mama taka cheza”
“Sawa kacheze nje”
“Chawa”
Uzuri wa Abraham ulitingisha mtaa mzima na kila aliyemuona mtoto huyo alitamani ambebe,ingetokea angevalishwa sketi ungesema kuwa ni mtoto wa kike, kutokana na kulelewa vizuri kijijini hapo ilifanya apate afya nzuri na alinawiri,akazidi kuwa tetemesho!
“Mtui,nieleze”
Marietha akarudi tena na kuanza mjadala upya.Mtui hakuwa na sababu ya kuweka kitu chochote kifuani kwake sababu Marietha alitakiwa gerezani hivyo ilibidi afunguke kwa kusema yote yaliyompata Deo,alianza mwanzo mpaka mwisho hakuacha kitu chochote kile njiani.

Ilimchukuwa Mtui dakika arobaini na tano nzima mpaka kumaliza kila kitu na kuhitimisha kuwa Marietha anahitajika kwa wudi na uvumba ndiyo maana akafunga safari kutokea jijini Dar es salaam mpaka mkoani hapo.Kila mtu alishusha pumzi ya kuchoka,Marietha alishtuka kwani hakutegemea hata siku moja kuwa mtu kama Deo sehemu inayoitwa Segerea angewekwa,aliamini kwa pesa zake na umaarufu wake jambo hilo lingempita mbali hakujua kwamba sheria ni msumeno inakata kotekote!Kitu kilichomjia kichwani ni jinsi alivyomuweka Issa kituo cha polisi miaka mingi iliyopita akimtuhumu kuwa ni mwizi na sasa Issa ni tajiri wa kufa mtu!
Hapo ndipo alipoamini kuwa dunia ni duara na malipo ni hapahapa duniani,alitafakari vitu vingi sana akawa kama anaangalia mkanda wa filamu kichwani kwake.
“Marietha tafadhali,twende Dar es salaam”
Mtui akazidi kulisisitizia jambo lililompeleka mkoani hapo.Sio siri alikuwa njiapanda hakuelewa ni kitu gani akifanye,moyo wake ulimsukuma aende Dar es salaam lakini upande wa pili wa nafsi yake uligoma katukatu kwani alivikumbuka vituko na manyanyaso ya Deo, hiyo ilitosha kabisa kumfanya asite.
“Marietha”
Sauti ya Mama yake mdogo aliyeitwa Vaileth ilisikika,huyu ndiye alikuwa mkubwa kuliko wote na mwenye busara sana.
“Abee Mama”
“Deo ni mumeo na mlifunga ndoa ya Kikristo.Mlikula kiapo Kanisani,tafadhali nenda kamuone Mumeo.Anahitaji kukuona”
“Hapana Mama siwezi”
“Mimi nakuomba Mama yako,jifunze kusahau.Kubali kwanza wito”
“Mama bado moyo wangu ni mzito”
“Legeza Mwanangu”
Haikuwa kazi rahisi kwa Marietha kukubali jambo hilo hata kidogo lakini kutokana na shinikizo la wengi ilimuwia vigumu kuchomoa, hatimaye akakubali na hapo hakukuwa na kipingamizi kingine chochote kile.
“Alisema anahitaji kumuona Abraham pia”
Mtui akasema alivyomuona Marietha ameweka mabegi yake tayari kwa safari.
“Hilo halitowezekana”
“Nakuomba”
“Nisingependa Abraham ajuwe hili,sitaki ajuwe Baba yake yupo gerezani”
“Sawa”
Ilikuwa tayari imetimu saa mbili ya usiku ingawa Mtui aliambiwa apumzike kisha kukikucha ndiyo aanze safari lakini aligoma na kutaka arudi siku hiyohiyo Dar es salaam na kutokana na uwezo wa gari yake kubwa aliamini ingemfikisha jijini Dar es salaam sio chini ya masaa manne,walivyoingia ndani ya gari safari ilianza mara moja.
Walivyofika Chalinze Mtui alisimamisha gari na kuliweka kando!
“Utakula nini?”
“Sijisikiii kula”
Marietha alijibu lakini Mtui alivyotoka nje ya gari baada ya dakika tano alivyorudi ndani ya gari alikuwa ameshika mfuko unaonukia nyama za kuchoma pamoja na soda za kopo.
“Chukua mfuko huu,kula Shemeji”
“Ahsante”
Kutokana na harufu nzuri ya nyama ya mbuzi za Chalinze ilimfanya Marietha aufakamie mfuko na kuanza kusosomola nyama moja baada ya nyingine huku safari ikizidi kuendelea.
Hesabu za Mtui zilikuwa ni kufika Dar es salaam kabla ya saa sita na hivyo ndivyo ilivyokuwa sababu aliingia nyumbani kwake Tegeta kwa ndevu saa tano na dakika ishirini na saba,akaweka gari nje ya nyumba yake na kupiga honi ambapo geti lilifunguliwa na mlinzi wa kimasai.
“Karibu nyumbani kwangu”
Ilikuwa ni nyumba ndogo lakini nzuri mno.
“Ahsante”
Mtui alivyoshuka ndani ya gari akamuita Masai wa getini ili asaidie baadhi ya mabegi na kuyaweka ndani.
Baada ya kuingia ndani Marietha alionyeshwa sehemu ya kulala na chakula kilikuwa kimeandaliwa mezani tayari na mfanyakazi wa ndani.
“Jisikie huru…..Deboraaaaa”
Mtui akamuita dada wa kazi.
“Huyu ni shemeji yangu.Atakaa hapa naomba umuangalie vizuri”
“Sawa Baba”
“Kaendelee na kazi”
Siku hiyo sijui ilikuwa bahati mbaya ama nzuri sababu mke wa Mtui hakuwepo na alisafiri kwenda mkoani kwao Morogoro kuwasalimia wazazi wake lakini habari za Marietha kuwepo nyumbani kwake alizijua kwani simu zilikuwepo ilikuwa ni lazima taratibu zote zinazoendelea hapo mama mwenye nyumba apewe habari yaani mke wa Mtui vinginevyo kingezuka kitimtim kwani Mke wa Mtui alikuwa mtata sana.
*********
Marietha aliendelea kuishi nyumbani kwa Shemeji yake Mtui kwa muda wiki moja kwa amani kabisa ambapo ulivyofika muda wa kuwaona wafungwa siku hiyo waliingia ndani ya gari asubuhi na safari ya kwenda gerezani kuanza mara moja.
Akiwa ndani ya gari muda wote alikuwa akitafakari vitu vingi sana,hakuelewa ni kitu gani atakifanya endapo akikutana na Deo mubashara yaani macho kwa macho siku hiyo.Gari likaingia lango la gereza na kupaki pembeni,wote wakashuka na Mtui alikuwa ana mifuko ya vyakula mikononi mwake,moja kwa moja akaenda mpaka kwa askari jela, kwa kuwa walimzoea walijuwa anamtafuta Deo Karekezi hivyo hakukuwa na haja ya kuhoji maswali.
“Deo Karekezi?”
“Ndio afande”
Askari Jela akasimama na kutembea ambapo alivyorudi baadaye pembeni alikuwa ameongozana na Deo Karekezi.
Moyo wa Marietha ulipiga kwa nguvu sana na alihisi kuishiwa nguvu za miguu ingawa hakujuwa ni kwanini hali hiyo inatokea mbali na hapo alijisikia kulia wakati huohuo,afya ya Deo ilimtisha sababu alikuwa amepungua uzito na mwili wake una magamba na mabakamabaka,alijisikia kumuonea huruma akashindwa kuvumilia akaanza kububujikwa na machozi ya uchungu yakapita mashavuni na kudondoka chini!


Marietha alibubujikwa na machozi kama mtoto mdogo,akaanza kulia kwa kwikwi ni dhahiri kuwa alijisikia uchungu uliozidi kipimo chake,vitu vingi vilianza kupita kichwani mwake hususani siku ya ndoa yao wakiwa kanisani wenye furaha mno ingawa Deo alimfanyia ubaya na kumnyanyasa lakini aliamini halikuwa kosa lake kwani hakuwa anaelewa lolote,mwili wa Deo ulikongoloka na afya yake ilipungua kwa kiasi cha kutosha hiyo ilifanya mpaka ngozi yake ijae ukurutu kumaanisha kuwa gerezani aliteseka sana.
“Marie…tha”
Deo akaita akiwa tayari ameshikwa na kwikwi hata yeye alishindwa kuvumilia, akajikuta analia machozi sababu hakutegemea kama Marietha angetokea,kwa picha iliyokuwepo ilifanya mpaka Mtui atoke pembeni sababu alihisi kulia nayeye, kingine kilichomfanya kutoka hapo alitaka awape faragha wanandoa hao wawili.
Deo na Marietha walikumbatiana na kuendelea kulia mtindo mmoja na hakuna hata mmoja kati yao aliyeweza kumtuliza mwenzake hali hiyo ilifanya askari jela wawatizame!
Siku hiyo ilipita bila kuongea lolote sababu muda wa kuona wafungwa uliisha na Deo akarudishwa gerezani,kumaanisha kuwa kumuona mpaka mwisho wa mwezi.Marietha aliumia moyo kupita kiasi.
Akatoka nje, huko walionana na Mtui kisha wote kurudi ndani ya gari ili safari ianze ya kurudi nyumbani.

Marietha aliishi kwa Mtui vizuri na alijisikia Amani kabisa,alivyotaka kuondoka kurudi mkoani kwao Tanga Mtui alimzuia, alitaka awe karibu ili iwe rahisi kwake kuonana na Deo.
“Kaa tu hapa kwangu,hakuna shida”
“Inabidi nirudi,nimewaacha wanangu Tanga”
“Unaonaje wakaja pia kuishi hapa sababu hata Deo akitoka gerezani ni lazima aje kuishi hapa kwanza mpaka mambo yatakapokaa vizuri”
“Lakini Sheme…”
“Marietha tafadhali,baki hapa nyumbani.Hapa ni nyumbani kwako pia,Deo ni ndugu yangu”
“Sawa lakini nataka kujua kitu kimoja”
“Kitu gani?”
“Nani amemfunga Deo?”
“Ni stori ndefu kidogo lakini ni mwanamke mmoja wa kihindi na Mumewe”
“Ilikuwaje?”
“Kama nilivyokwambia ni hadithi ndefu lakini nitakwambia kesho sasa hivi usiku umeingia.Maliza chakula”
Marietha alihudumiwa ndani ya nyumba ya Mtui kama Malkia na hata siku moja hakuwahi kudhani kuwa kuna binadamu wenye roho za huruma kama Mtui kama wapo basi sio Afrika wapo mahali fulani wenda Ulaya lakini hivyo ndivyo ilivyokuwa,siku zilizidi kusogea harakaharaka akiwa nyumbani kwa Mtui anasubiri mwisho wa Mwezi ufike ili akamuone Deo,aliapia siku hiyo angejikaza ili waweze japo kuzungumza.
“Leo nimeota ndoto mbaya sana Shemeji”
Siku hiyo Marietha alimwambia Mtui wakiwa wanakula chakula cha usiku mezani.
“Nini tena?”
“Nimeota,sijui nipo wapi lakini kwenye harusi ya mtu nimeingia nimeanza kufanya fujo”
“Mh,hizo ni ndoto tu.Acha kuwaza sana,bado wiki mbili tu twende tukamuone Deo”
“Sawa Shemeji Ahsante kwa kila kitu”
“Naomba pia uwalete na wanao hapa,wawe wanaishi na sisi”
“Ahsante”
“Usijali,mimi naenda kulala.Usiku mwema”
Mtui akaondoka na kumuacha Marietha seblen peke yake anamalizia kula kisha kila kitu kilivyoenda sawa alitoka na kuingia chumbani kwake ambapo huko alioga na kujitupa kitandani.
Kuanzia siku hiyo alikuwa kama mwanafunzi wa ‘boarding’ anayehesabu siku za kufunga shule ili aende likizo nyumbani kwani alikuwa karibu sana na Kalenda anaiangalia na kuhesabu siku zilizobaki ili akamuone mumewe gerezani,moyo wake ulihisi kumuona Deo na wala sio kitu kingine chochote kile! Siku hazigandi kwani mwezi ulikatika kimasihala masihala na hatimaye siku hiyo ikafika kama kawaida wakapitia kwenye migahawa mbalimbali ili kununua chakula cha kumpelekea Deo gerezani,Marietha alikuwa mwenye hamu kubwa sana ya kumuona Deo na hilo lilikuwa pembe la Ng’ombe halikuweza kufichika hata kidogo ndiyo maana muda wote alikuwa anamsihii Mtui atembeze gari kwa haraka ili wawahi kufika amuone tena Deo.
Walifika Gerezani saa sita mchana na kushuka ambapo mara moja walifika mapokezi na kuitiwa Deo.
Kama ilivyokuwa mara ya kwanza ndivyo ilivyokuwa siku hiyo,Marietha alianza kulia upya na kufanya Deo aanze kumwaga machozi kama mtoto mdogo.
“Mar..ieth..a usili..e nyama..za Mke wangu”
Deo alijaribu kumtuliza mkewe asifanye anachokifanya huku yeye akiwa anabubujikwa na machozi bado.
“De..o naku..penda Mume wa..ngu kwan..nini si..si!Tumem..fanya ni.ni Mungu,Naomba unisamehe kwa mambo yote niliyofanya”
“Nimekusamehe na nim..efurahi kuku..ona”
“Naku..pend.a Mume wangu”
“Mimi pia”
Hapo,walifuta machozi na kila mtu akawa anaongea kwa sauti lakini kwa kwikwi,Deo alitaka kujua hali ya Abraham inaendeleaje na alimshukuru Mungu mwanae anaendelea vizuri.
“Na mwingine yule jina lake nani,hali yake?”
Alimaanisha mtoto wa kizungu.
“Anaendelea vizuri”
“Jina lake nani?”
“Bado sijam…pa ji…na”
“Usilie Marietha nyamaza,nakupenda na ninampenda pia mtoto wako.Ni wangu pia sababu wewe ni mke wangu,Kanisani tulikula kiapo kifo ndiyo kitatutenganisha na sio binadamu yoyote yule,mimi nawewe mpaka kifo”
Maneno hayo yalimtoka Deo kutoka ndani ya shina la moyo wake na alimaanisha kutamka anachokisema sababu hakutaka kukumbuka maisha yake ya nyuma aliyopitia, kivyovyote aliamini mke wake ndiyo kila kitu na Mtui ndiye ndugu yake wa kufa na kuzikana sababu hata siku moja hakuna mtu mwingine yoyote yule aliyefika kumuona.
Siku hiyo walizungumza vitu vingi sana na Marietha alitaka kujua nini kimetokea mpaka Deo amefungwa gerezani.
“Nilibambikiwa pesa feki”
“Kivipi Mume wangu?”
“Nilikuwa nadaiwa pesa nyingi sana,ikabidi niuze saluni.Wateja niliopata wakanunua kumbe pesa zile zilikuwa feki na anayenidai hakutaka kunisikiliza,akaniweka ndani basi ikaanzia hapo.Ilibidi wataifishe nyumba na magari yangu yote.Kampuni imekufa pia naweza kusema waliokuwa wananidai ndiyo walishinikiza mimi nifungwe”
Deo alisimulia kila kitu na Marietha alikuwa makini sana kumsikiliza kila nukta ya neno analozungumza.
“Akashindwa kukuonea huruma huyo anayekudai?Sio ubinadamu siwezi kuamini kama kuna Watanzania wenye roho kama hizo”
“Sio mtanzania ni dada wa kihindi”
“Mbona wahindi wana roho nzuri.Ni nani?”
Marietha alikumbuka wema aliofanyiwa na Katrina hivyo alichukulia wahindi wote ni wastaarabu na hakuelewa kuwa ndiyo huyohuyo aliyechangia kumuweka Deo gerezani.
“Ni binti fulani hivi,Mtui anamfahamu ni dokta pale aghakhan”
“Inabidi niongee naye”
“Hapana usijlali Marietha,nishahukumiwa tayari”
“Hapana Deo hata kama”
Ingawa hakuelewa ni namna gani sheria zinavyokwenda lakini alijisikia kuonana na mwanamke huyo wa kihindi aliyemweka gerezani mumewe.
“Mimi sina shida,fanya unachojua”
“Sawa Deo,nakupenda na nitaendelea kukupenda mpaka pale kifo kitakapotutenganisha.Wewe ni wangu wa Maisha”
Marietha alizungumza maneno hayo kwa hisia kali sana na ndani yake hakukuwa na punje ya masihala hata kidogo,bila aibu yoyote akamsogelea karibu Deo na kuanza kumnyonya mdomo yaani denda.
“I love you”(Nakupenda)
“Mimi pia.Lakini nahitaji kumuona Abraham wakati mwingine ukija njoo naye”
“Sawa mume wangu”
Siku hiyo moyo wake ulikuwa mwepesi sana na alihisi kama kuna kitu kizito amekitua kutoka ndani ya moyo wake.
Muda wa kuona wafungwa ulivyoisha alianza kuumia tena moyo sababu alitamani Deo awe naye muda wote wanazungumza ikiwezekana utokee muujiza awe huru mara moja lakini ndiyo hivyo, hakukuwa na namna nyingine ya kufanya zaidi ya kukubali matokeo!
Waliondoka na Mtui jioni ya saa kumi na moja mpaka Tegeta ambapo huko alifika na kujimwagia maji bafuni,akafika seblen na kumkuta Mtui anaangalia televisheni.
“Shemeji”
“Naam”
“Nahitaji kuonana na huyo dada wa kihindi.Lini utanipeleka?”
“Kumbe ulikuwa siriazi?”
Mtui akajibu kwa swali.
“Ndio,hata ikiwezekana kesho nipeleke”
“Basi sawa,Kesho jioni lakini mumewe mkali sana nadhani ndiyo kafanya mpaka Deo yupo gerezani”
“Ahsante sana,mimi nitazungumza nao wote”
Marietha hakutania kwani siku iliyofuata alimkumbusha Mtui asubuhi na mapema akimsisitiza kuwa jioni yake ampeleke nyumba ya dada wa kihindi aliyeshinikiza mpaka Deo afungwe gerezani.
“Jioni nikirudi tutaenda wote”
“Sawa shemeji kazi njema”
“Aya ubaki salama”
Kichwani kwa Marietha kulimiminika vitu vingi sana siku hiyo na alitafakari mambo mengi juu ya maisha yake ambayo aliyafananisha na sinema ya kusisimua mno na kama angeichezea sinema basi ingeuzwa mno!Sekunde kwake siku hiyo ilisogea kwa mwendo wa kinyonga lakini hatimaye jioni ikafika akasikia honi ya gari,akakurupuka kutoka kwenye kochi sababu alijua Mtui tayari amefika hivyo alitoka nje.
“Naona ulikuwa unanisubiri sana”
Mtui akaanzisha maongezi baada ya kushuka ndani ya gari.
“Ndiyo nilikusubiri kweli”
“Pole ngoja basi nioge nibadili nguo maana nanuka jasho”
“Sawa,namimi basi naenda kujiandaa”
Hivyo ndivyo mambo yalivyokwenda na baada ya dakika kumi na mbili kila mtu alikuwa tayari kabadili nguo wakaingia ndani ya gari na safari ya kwenda Mbezi kuanza hapohapo,Kwa kuwa kulikuwa na njia ya mkato ilibidi waingie afrikana ili watokee Mbezi ya Chini,ilikuwa ni lazima wafupishe njia ili wafike Mbezi Beach nyumbani kwa mwanamke wa kihindi,safari ilizidi kusonga mbele lakini Marietha alianza kufikiria vitu vingi sana sababu mitaa waliyokuwa wanapita ilimkumbusha kitu.
“Labda sio huku”
Mara ya mwisho kufika mitaa hiyo ilikuwa ni kupewa msaada na muhindi aliyekuwa na uhusiano wa kimapenzi na Issa,jambo hilo lilimjia kichwani hapohapo lakini aliomba Mungu isiwe hivyo.Moyo wake ukapiga paaa! Baada ya gari la Mtui kusimama nje ya geti kubwa la kisasa la rangi nyeusi,nyumbani kwa Katrina.
“Pi piiiiiiii”
Mtui akapiga honi.
“Kuna watu wana uwezo bwana,hili geti la kisasa hapa halifunguki yaani hili geti linatambua magari ya mwenye nyumba tu,gari likifika hapa geti linafunguka lenyewe”
“Hapa ndiyo kwa huyo Muhindi?”
Marietha akauliza,mambo ya geti hayakumuhusu.Na nyumba hiyo aliikumbuka sababu Issa na Msichana wa Kihindi ndio walikuwa wakiishi humo.
“Ndio hapa”
Baada ya jibu hilo alihisi uti wake wa mgongo umepigwa na ubaridi wa ghafla.
“Pii piiiiiiii”
Akapiga tena honi lakini wapi,hakuna mtu yoyote yule aliyefungua geti.Ilibidi Mtui ashuke na kumsimamisha kijana mmoja anayepita njia.
“Kaka samahani kidogo”
“Bila samahani kiongozi”
“Naomba kuuliza,hawa watu wa humu wako wapi?”
“Mimi sio mwenyeji”
“Sawa”
Mtui akatembea mbele kidogo mpaka kwenye duka moja la vyakula vya jumla na kusema shida yake,Marietha alikuwa nyuma yake.
“Mnamuulizia yule dokta Katrina?”
“Ndio huyo Yes,huyohuyo”
“Alikuwepo hapo lakini ameenda kwenye mazishi leo asubuhi”
Moyo wa Marietha ukapiga paaa!Lakini hakuelewa ni kwanini kashtuka namna hiyo.
“Samahani kaka angu,nani amefariki?”
Marietha akauliza kwa kiwewe!



Hata kabla hajajibiwa mapigo yake ya moyo yalikuwa yakizidi kupiga kwa nguvu,akahisi kama mwili wake umeanza kufa ganzi mbali na hapo alitamani alichokiwaza kichwani kwake kiwe tofauti kabisa ndiyo maana aliganda akimuangalia Mwanaume aliyesema kuwa Katrina kapata msiba na ameondoka,akili yake ilimtuma kuwa ni Issa wenda ndiye amefariki ingawa fikra hizo alizitupilia mbali na kuziita za kishetani.
“Mchele gunia moja shilingi ngapi?”
Ni mteja ndiye aliyemkatisha muuzaji vyakula kutoa jibu, hiyo ilimkera sana Marietha moyoni mwake.
“Hili la kilo mia?”
“Ndio”
“Laki mbili”
“Sasa em….”
“Kaka samahani hujanijibu”
Marietha aliingilia kati alivyoona anacheleweshwa hakuwa mwenye staha hata kidogo.
“Ngoja nimuhudumie mteja dada angu”
“Sasa si unijibu tu nani kafariki kwani itachukuwa dakika ngapi?”
Marietha aliuliza safari hii sura yake ilikuwa imejikunja kiasi, tena aliambatanisha na ukali mno hiyo ilimshangaza sana Mtui aliyekuwa pembeni yake hakuelewa ni kwanini Marietha anamkaripia muuza vyakula huyu.
“Marietha”
Akaita na kumsogeza pembeni.
“Mtui nataka kujuwa ukweli”
“Ukweli gani?Kuna mtu yoyote hapa unamfahamu?”
“Ndio,hapana”
Akababaika kidogo,hakutaka Mtui ajuwe chochote sababu ungeanza tena mjadala mwingine jambo ambalo hakutaka litokee kabisa.
“Shemeji embu ngoja kwanza”
Marietha akatoka kwa Mtui na kurudi tena moja kwa moja mpaka kwa muuza mchele na vyakula.
“Kaka samahani,hukuniambia nani amefariki”
Lilikuwa ni swali lilelile.
“Ni mjomba wake na Dokta Katrina alikuwa jela,alijinyonga akiwa hukohuko.Juzi ndiyo kulikuwa na msiba hapa”
“Kwanini alifungwa sasa?”
“Mimi sijui lakini nilisikia alimpa sumu mume wa Katrina,hiyo inshu hukusikia wewe dada?Ilivuma sana hapa mtaani”
“Mume wake ndiye aliyewekewa sumu?”
“Ndiyo,yaani binadamu ni wabaya sana.Wahindi waligoma hawakutaka aolewe na muafrika”
“Huyo mume wake anaendeleaje?”
“Wewe dada nawewe Shilawadu sana!Kila kitu unataka kujua.Mimi sijui huyo jamaa anaendeleaje lakini mwezi uliopita alikuwa ana hali mbaya sana”
Marietha alihoji maswali siku hiyo kama polisi na Muuza duka aliyajibu bila kuchoka,nyuma alikuwa amesimama Mtui anasikiliza kila kitu.
Hiyo haikufanya Marietha asitishe zoezi lake la kumsaka mwanamke wa Kihindi ambaye alijuwa anaitwa Katrina mbali na hapo alishaelewa kuwa Issa ndiye aliyeshinikiza mpaka Mumewe awepo gerezani ni wazi aliamini nyuma yake kuna kisasi.
“Siwezi kukubali lazima niongee na Issa,kivyovyote vile ili Deo atoke.Hawezi kumfanya mume wangu anateseka gerezani namimi nipo hai,nitapambana naye mpaka dakika ya mwisho”
Siku hiyo Marietha akiwa kitandani anausaka usingizi alikuwa akitafakari,akachukuwa muda huo kukumbuka vitu vyote vya nyuma vilivyopita,akakumbuka jinsi walivyokuwa wanaishi na Issa kisha akatokea Deo akamuingia ndani ya moyo wake,wakafunga ndoa wakawa mume na mke na baadaye kuzaa mtoto kisha baadaye matatizo makubwa yalimkumbaa baada ya kwenda nchini Paris na kubakwa na Amadour.Hiyo ilikuwa ni historia tosha ambayo ingefaa kuandikiwa simulizi ya kusisimua.

Asubuhi kulivyokucha kama kawaida,Mtui akamgongea mlango kuwa anaondoka na kuelekea kwenye pilika za kutafuta mkate.
“Mimi naondoka Shemeji”
“Aya shemeji,mimi bado nipo”
“Sawa,chochote kitakachotokea mwambie dada anipigie simu”
“Sawa shemeji”
Mtui akiwa amesimama nje ya mlango Marietha yupo ndani ya chumba walizungumza na hiyo ndiyo staili waliyokuwa wanatumia kuwasiliana.
Akili ya Marietha hapohapo ikafanya kazi kwa haraka kama kompyuta isiyokuwa na mafaili,akaingia bafuni harakaharaka na kujimwagia maji,akaenda kwenye begi lake la nguo na kutoa nguo zake na kuvaa,ilikuwa ni lazima siku hiyo afunge safari mpaka Mbezi beach akaonane na Katrina ama Issa ikibidi!Ndiyo maana alivaa nguo zake harakaharaka,haikuwe­zekana hata siku moja yeye kubaki uraiani alafu mumewe awe gerezani anateseka,aliamini kuwa Katrina ni msichana mwenye roho nzuri sana hivyo ilikuwa ni lazima amwingie.Akachukuwa pesa kidogo ambazo alikuwa nazo kama akiba na kutoka mpaka seblen!
“Natoka kidogo dada”
“Sawa,nipike mchana utarudi?”
“Ndio nitarudi, sitochelewa”
Alivyohakikisha ameaga akafungua mlango na kutoka nje ambapo huko alitafuta daladala za Ubungo,bahati nzuri alipata siti na kukaa.Kichwani kwake kulikuwa na mawazo chungu mzima, mpaka anafika Ubungo na kupanda basi la Mbezi ilikuwa hivyohivyo,bahati nzuri alifika na kuanza kutembea mtaa kwa mtaa mpaka alipofika daraja la Malesela,akavuka barabara na kuipita supamaket.
Hiyo ilimaanisha bado mita chache tu akumbane na nyumba anayoishi mpenzi wake wa zamani Issa Nurdin Mpelembe.Ni kweli,alitembea mpaka getini na kuanza kugonga!Japokuwa hakuwa ana uhakika kama kuna watu ndani lakini alifanya tu kujaribu.
Katika kugonga geti,alishtuka baada ya kusikia muungurumo wa gari kisha geti lenyewe kufunguka bila mtu yoyote yule kulifungua hiyo ilitokana na gari kulifikia geti.Lilikuwa ni gari la kifahari aina ya BMW X5 vioo vyeusi yaani tinted!
Likasimama hapohapo ingawa geti lilikuwa wazi, ilionekana mtu aliyekuwa anaendesha gari alitaka kuzungumza naye na ndivyo ilivyokuwa kwani kioo cha gari upande wa dereva kilianza kushuka taratibu,sura ya msichana mrembo wa kihindi ilionekana akiwa nyuma ya usukani,alikuwa ni Katrina.
“Shikamoo dada”
Marietha akasalimia ingawa alijuwa kivyovyote vile yeye ni mkubwa kuliko Katrina!
“Hujambo,nakukumbuka?Za siku nyingi?Karibu ndani”
Katrina alimchangamkia na kuongea maneno hayo,Marietha akaanza kutembea kuingia ndani huku nyuma gari likiingia pia.
“Karibu,za siku nyingi.Hivi unaitwa nani tena?”
Kumbukumbu za Katrina zilikuwa zinaingia na kupotea,sura ya Marietha haikuwa ngeni ndani ya memori kadi yake ya kichwani, sura hiyo ilikuwepo lakini mafaili hayakukumbuka jina lake.
“Marietha”
“Oooh Mariethaaa,karibu”
Katrina na Marietha wote wakaingia ndani ya nyumba!Macho ya Marietha yalikumbana na sable kubwa iliyonakshiwa na vitu vya gharama sana ingawa alishawahi kufika eneo hilo lakini siku hiyo vitu vingine vilikuwa vigeni kwake,alivyoangalia ukutani akahisi moyo kumuuma lakini hakujuwa ni kwanini,picha ya Issa ilikuwa ukutani akiwa amekumbatiana na Katrina na nyingine ndiyo kabisa walikuwa wamenyonyana midomo,bado hakutaka kuamini kwamba kufumba na kufumbua Issa amekuwa bilionea namna hiyo na ndiye huyohuyo aliyemfunga mumewe Deo na kumfilisi mali zake zote.
“Hizi ni mali za mume wangu,lazima zirudi tu”Aliwaza!
Kwa akili yake na upeo wake wa kufikiri alidhani wenda Issa alimfilisi Deo kwa makusudi,ndiyo maana akajenga jumba kubwa kama hilo na kuendesha magari ya kifahali huku Deo akiwa anasota gerezani.
“Nina mazungumzo nawewe”
Marietha akavunja ukimnya.
“Sawa nakusikiliza,have a seat”
“Ahsante”
Marietha akakaa na Katrina akaketi ili mazungumzo yaanze.Kwa Marietha kwake ulikuwa mtihani mkubwa sana sababu hakuelewa ni wapi aanzie.
“I’m listening”(Nakusikiliza)
Ilibidi Katrina aanzishe mazungumzo baada ya kuona Marietha yupo kimnya lakini ndani ya moyo wake alikuwa na chembechembe za wivu kutokana na historia ya Marietha na Issa,ndiyo maana alianza kujibu kwa mikato ingawa alipachika tabasamu la bandia usoni.
“Ninaweza kuzungumza na Issa?”
“Issa?Kwanini?Una shida naye gani?Unaweza ukasema hapahapa”
“Anaendeleaje kwanza?Nilisikia yupo hospitali”
Hapo ndipo moyo wa Katrina uliumia, hakuelewa Marietha alipozitoa habari za Issa,ndiyo maana akakunja sura kidogo ingawa hakutaka jambo hilo alioneshe waziwazi.
“Tunafunga ndoa next Month”Akabadili mada niya yake ilikuwa ni kumtia wivu.
“Hongereni”
“Ahsante lakini sijajua bado kilichokuleta hapa nyumbani”
“Ningependa kuongea na Issa lak…”
“Subiri kidogo nipokee simu”
Katrina alimkatisha Marietha kwani simu yake ilikuwa inaita,ilikuwa ni lazima aipokee sababu ilitoka hospitalini kwa daktari ambaye anamtibu Issa,hapohapo akaipokea na kuiweka sikioni.
“Yes Halloo,ndio anaendeleaje?Aaah aaah!Anaongea sasa,anataka kuniona?Ahsante Mungu.Allah abdulilah….Nakuja sasa hivi jamani.Thank you God”
Katrina alikata simu akionesha tabasamu mwanana, ilielekea simu aliyopokea ilisababisha awe na furaha.
“Samahani kidogo,unaweza ukaja Kesho.Ama nakupa namba zangu unitafute”
“Nitakuja tu kesho”
“Ahsante”
Katrina aliingia chumbani kujiandaa mbiombio huku Marietha akitafakari jinsi ya kuondoka.
*********
Katika watu ambao waliookoa maisha ya Issa kwa asilimia kubwa ni Dokta Khaila ambaye muda wote alikuwa anawapeleka puta madaktari wake wasifanye uzembe kwani aliwaambia endapo uzembe wowote ungejitokeza ama Issa angepoteza maisha basi wangekiona cha mtema kuni,kauli hiyo iliwafanya kuhaha na usiku kucha madaktari walipishana wodini kwa Issa wakimpatia matibabu ingawa waliamini kuwa maisha ya Issa yapo mikononi mwa Mungu peke yake.Walijitahidi kupambana mwanzo mpaka mwisho sababu hali ya Issa haikuwa nzuri hata kidogo,ndiyo maana kila daktari alihaha kuliko kawaida.Kila siku walimpelekea taarifa mbaya Dokta Khaila pamoja na Katrina.
“Nambie ukweli,Issa yupo hai au keshakufa?Nambie ukweli Sharif”
Dokta Sharif koti lake lilikuwa limekunjwa kunjwa na Katrina aliyeonekana akiwa mwenye hasira na uchungu wa kutaka kujua hali ya mpenzi wake Issa.
“Taratibu Katrina,utanichania koti langu.Issa yupo salama lakini bado hali yake sio nzuri”
“Naweza kumuona?Unanidanganya”
“Hapana ni kweli na kwa sasa huwezi kumuona”
“Kwanini sasa?”
“Bado hana fahamu na kelele haziruhusiwi”
Huo ndio ulikuwa mzozo mkubwa baina ya Katrina na dokta Sharif baada ya kutoka ndani ya chumba cha Issa.
Siku zilizidi kwenda lakini hakukuwa na mabadiliko yoyote yale kwa Issa.Hiyo haikufanya apoteze matumaini, kila siku Katrina alikesha hospitalini akilia machozi,alivyokumbuka ndoa yake ambayo aliipania alizidi kuumia mtima zaidi.
Siku moja akiwa juu ya benchi alimuona Mama yake ameshikilia simu na baada ya hapo sura yake ilibadilika,kuna jambo halikuwa sawa ikabidi asimame kwa haraka na kumuendea,hapohapo akahoji.
“Baba yako mdogo kafariki,kajiua akiwa maabusu”
“Mungu wangu”
“Ndio hivyo”
Zilikuwa ni habari mbaya kwa kila mtu ingawa mtu aliyekufa walimlaani kwa kutaka kujaribu kumuuwa Issa.Ilibidi wafanye taratibu za kwenda kuuchukuwa mwili wa ndugu yao hospitalini kwa ajili ya kuuzika ambapo baada ya siku moja mbele ndugu jamaa na marafiki waliitwa ili wauchome moto mwili kama taratibu za kihindi zilivyokuwa mtu akifa!Na hivyo ndivyo walivyofanya.
Na Katrina alivyotoka kwenye mazishi akanyoosha moja kwa moja hospitalini kumuona Issa,hali yake ilikuwa vilevile.
“Katrina nenda nyumbani kapumzike,uoge”
“Lakini Mama nataka kubaki hapa hospitali”
“Nakuomba Mwanangu Issa atapona”
“Okay”
Kwa unyonge akaondoka na kurejea nyumbani kwake akiwa hoi bin taaban!
*******
“Katr…ina..Naku…penda Katr..ina Katri..naaaaa”
Ilikuwa ni sauti iliyosikika kwa kukwaruza na kwa mbali sana kutoka juu ya kitanda alicholazwa Issa akiwa amezungukwa na mitungi ya hewa ya Oksijeni, kwa mara ya kwanza Madaktari walishtuka sababu hawakutarajia kama muujiza wa Issa kuongea ungetokea,Wote wakasogea kwa haraka mpaka alipo.
“Isaa”
“Katr…ina”
Issa aliendelea kuita huku akianza kufumbua macho yake taratibu,hayo yalikuwa kama mazingaombwe sababu hakuna hata daktari mmoja aliyedhani kuwa Issa angepona.Kutokana na hekaheka za ndani ya wodi ilifanya Mpaka Dokta Khaila nayeye aingie,hakuamini alichokiona!Issa alifumbua macho yake na alikuwa akiangalia huku na kule.
“Mama,..Katr..ina yuko wapi?”
“Anakuja,pumzika usiongee”
“Nahi..taji kuzungumza naye”
“Anakuja”
Dokta Khaila alitoka mpaka nje na kuchomoa simu yake mfukoni na kumuendea hewani binti yake Katrina ili kumpasha habari nzuri zilizotokea,bahati nzuri alimpata hewani na kilichotokea kwa Katrina ni kukatisha maongezi na Marietha,akaaga akiwa mwenye furaha kupitiliza.
Alivyojiandaa akaingia ndani ya gari harakaharaka na kuligeuza kwa kasi,geti lilivyofunguka akalitoa mkuku kama mtu mwenye haraka ya kuwahi mahali fulani.Pembezoni mwa barabara alikutana na Marietha anatembea kwa miguu,moyo wake ulijisikia kumsaidia kumpakia ndani ya gari lake ingawa alikuwa mwenye haraka,hapohapo akaweka mguu kati gari likasimama akateremsha kioo!
“Ingia kwenye gari nikusogeze mpaka kituoni”
“Ahsante”
Marietha akafungua mlango na kuingia ndani ya gari ambapo safari ilianza dakika hiyohiyo.
“Kwanini mmeamua kumdhulumu mme wangu na kumuibia mali zake?NITALIPIZA KISASI”
Marietha aliropoka kwa hasira huku akimtizama Katrina kwa macho makali yaliyojaa chuki mno na aliongea akimaanisha,hiyo ilimfanya Katrina ashtuke kidogo na kugeuza shingo yake kumuangalia Mwanamke huyu anayeropoka bila kujuwa mali alizokuwa nazo amezitoa wapi.



Sio kosa lake,wenda shule ilimpitia kushoto ndiyo maana aliropoka bila kufanya utafiti wa aina yoyote ile, hakuelewa anaongea na msichana aliyezaliwa na kukuta wazazi wake wana mali nyingi sana.Kutokana na mambo yalivyoenda,Deo kufilisiwa ikiambatana na kufungwa na wakati huohuo Issa kuwa tajiri ilimfanya ajumuishe tukio hilo kama dhuluma!Akiwa ndani ya gari alizungumza vitu chungu mzima.
“Mkaona haitoshi mkaamua kumfunga jela,sheria itafuata mkondo wake”
“Unasemaje?”
Katrina akahoji na kupunguza mwendo wa gari lake sababu alihisi wenda anasikia vibaya.
“Kama nilivyokwambia,kwanini umeamua kumfunga mme wangu?Na mkamchukulia mali zake zote?”
“Deo ni mumeo?”
Swala hilo lilikuwa geni kwa Katrina ndiyo maana akahoji kwa hamaki.
“Unajifanya hujui au?”
“Ndio najua sasa hivi.Pole sana”
Ingawa Marietha alikuwa anaongea akionekana mwenye hasira lakini kwa Katrina yeye alijibu kawaida kwani hakutaka furaha yake ya Issa kupona imezwe na mwanamke huyu Marietha anayeongea hovyohovyo kama redio mbovu.
“Katrina naomba unisaidie”
“Nikusaidie nini?”
“Mme wangu yupo gerezani”
“Mmeo tapeli sana,alitaka kuniibia mali zangu”
“Hapana nyie ndio mmemzulumu mali zake.Wewe na Issa”
“Ishia hapohapo,ukitaka kunitibua muongelee Mme wangu”
“Nakwambia ukweli”
“Shuka ndani ya gari langu,sasa hivi”
Katrina hakuweza kuvumilia tena maneno anayoongea Marietha ndiyo maana akaweka gari kando na kumtaka ashuke,ni wazi kuwa aliyavumilia maneno mengi kutoka kwake kifupi alimstahi tu kwani kwa msichana ama mwanamke wa kawaida asingethubutu kuongea na Marietha.
“Issa hakutaki tena,shuka upesi”
“Wacha nikuoneshe kuwa OLD IS GOLD”
Marietha akateremka ndani ya gari akimalizia sentensi ya kiingereza akimaanisha kuwa cha zamani ni dhahabu, jambo ambalo lililozidi kumfanya Katrina avimbe kama chura, alitamani kushuka ampe vipande vyake.
“Stupid”(Mjinga)
Alitukana tu na kupiga gia,gari likateleza akaondoka zake ili awahi hospitalini Aghakhan akaonane na Issa wake,alihisi kujuta kuzungumza na Marietha kwani alimuharibia siku yake tayari.
Siku zote msichana huyu wa kihindi alikuwa ni mwenye wivu kuliko kawaida na moyo wake ulianza kumuuma akihisi kwamba ipo siku moja Issa na Marietha watarudiana,akiwa kwenye gari aliendelea kusongwa na mawazo.Ilikuwa wazi kabisa mfano Issa angekuwa ana fahamu ama hajapatwa na matatizo siku hiyo basi angekumbana na mvua ya maswali isiyoisha,aliwasili hospitalini saa saba ya mchana akapaki gari na kushuka harakaharaka ambapo alinyoosha moja kwa moja mpaka kwa Dokta Sharif.
“Issa yuko wapi?Anaendeleaje?”
Katrina akahoji maswali mawili tofauti, hiyo ilimfanya Dokta Sharif ashindwe kuanza kujibu swali lipi!
“Yuko I.C.U bado,lakini hali yake ni nzuri.Baadaye anaweza kuhamishwa”
“Ahsante”
Kwa mara ya kwanza tangu Issa aingie hospitalini hapo Katrina alionekana akitabasamu kwani habari hizo kwake zilikuwa njema kuliko kawaida,taratibu zilikuwa ni zilezile kuingia I.C.U ni lazima uvae nguo maalum,akavaa kisha kuvua viatu,alivyoingia tu akakumbana na Issa amefumbua macho,mtungi wa gesi ya oksijeni upo kando hiyo ilimaanisha kuwa anaweza kuvuta hewa bila msaada wowote ule wa mashine.
Ulikuwa ni muujiza mkubwa sana ambao hakutarajia kama ungetokea,kwa furaha aliyokuwa nayo bila kujali kuwa Mama yake yupo pembeni ama madaktari akamfuata Issa hapohapo juu ya kitanda na kuinama kidogo ambapo alisogeza mdomo wake karibu,midomo yao ikagusana Katrina akatoa ulimi wakaanza kunyonyana denda kwa kama sekunde tano nzima.
“I love you Issa,Mungu ni mkubwa”
Moyoni kwa Katrina kulijaa mapenzi tele dhidi ya mwanaume huyu,alikuwa ana sababu zaidi ya milioni za kumpenda Issa kama ingetokea angeulizwa ni kwanini anampenda Issa namna hiyo kwani aliamini kama yeye chanda basi Issa ni pete!
“Unajisikiaje Darling?”
Katrina akauliza huku akiwa karibu kabisa na Issa.
“Sa..sa nipo poa tu!Lakini bado nasikia maumivu kifuani”
“Usijali utapona,Mungu ni mkubwa sana”
“Nini kilitokea?”
“Ulikunywa kitu chenye sumu”
“Mimi?”
“Ndio love lakini uliwekewa kwenye maji”
Katrina hakuficha kitu chochote kile, ilibidi amuhadithie kila kitu na kumpa habari kuwa aliyemuwekea sumu tayari amefariki dunia,bado Issa hakuamini kwamba amepona tena.Mkasa huo ulifanya akili yake isafiri na kujiona miaka mingi iliyopita jinsi alivyokuwa anawindwa na baba yake mkwe Marehemu Kapoor, hiyo ilimfanya aamini kuwa bado kuna watu wanamuwinda lakini pia aliamini kwamba Mungu wake bado anampigania.

Hali ya Issa ilifufua tumaini jipya ndani ya moyo wa Katrina kutokana na kwamba aliendelea vizuri,aliweza kuongea na kutabasamu tofauti na hapo awali,hilo lilikuwa jibu tosha kwamba maisha yataendelea vizuri ndiyo maana Katrina wakati wote meno yake yalikuwa nje anacheka kila wakati.
Taratibu za kumtoa Issa ICU zilianza mara moja ambapo alipelekwa wodi lingine kwa ajili ya vipimo vidogo vidogo kisha baadaye aruhusiwe.Na hilo aliliomba Katrina siku hiyo.
“Si anaweza kuruhusiwa leo?”
Lilikuwa ni swali lililorudiwa mara tisa kutoka kwa Katrina akiwagasi madaktari wodini kwao, ilikuwa kero lakini wangefanya nini?Wakati ni mtoto wa bosi wao!
“Ndio ataruhusiwa leo,Sumu yote imeisha lakini subiri tumfanyie kipimo cha mwisho”
“Kwahiyo mkimfanyia kipimo cha mwisho,nitaweza kurudi naye nyumbani?”
Katrina akarudia kitu hikohiko kukiuliza kwa mara nyingine tena!
“Ndio Katrina”
“Sawa ahsante”
Dokta alivyotoka nje ya wodi alilolazwa Issa,Katrina akasogea mpaka kwa Issa na kumshika mashavu akimuangalia mpenzi wake kwa jicho lililojaa husda na mahaba tele moyoni!
“Issa nakupenda sana.Ndoa yetu tufunge hata kesho kama ukiwa tayari”
“Mimi nipo tayari hata leo”
“Kweli baby?”
“Ndio mpenzi wangu?Nishapona tayari”
“Nakupenda sana”
Hakukuwa na haja tena ya madaktari kuendelea kubaki na Issa ndani ya hospitali baada ya majibu kutoka kuwa anaendelea vizuri,hivyo walimruhusu na alichofanya Katrina ni kutembea naye taratibu mpaka nje ambapo huko alikuwa amepaki gari yake,wakaingia na safari ya kuanza kurudi Mbezi beach kuanza na nyuma ya usukani alikuwa amekaa Katrina anaendesha gari kwa umakini sana kutokana na giza lilikuwa tayari limeingia.
Walivyofika Mwenge badala ya kunyoosha moja kwa moja Katrina alikunja kushoto na kuzidi kunyoosha mguu.
“Baby tunaenda wapi?”
“Marry Brown,kununua chakula”
“Okay”
Katrina alipaki gari nje ya jengo kubwa lililokuwa maarufu jijini Dar es salaam kama Mlimani City, hapo walishuka na kutafuta mgahawa mmoja ulioitwa Marry Brown.
“Nini dada nikuletee?”
Mhudumu msafi na mrembo alisogea karibu yao na kuwauliza.
“Mimi niletee baga na pepsi”
“Kaka”
“Hivyo hivyo”
“Baby nawewe kwa kuiga”
Katrina akaweka utani kidogo wote wakacheka!Walianza kula baada ya chakula kuletwa na walivyohakikisha matumbo yao yapo vizuri walisimama na kurudi ndani ya gari ambapo safari ya kwenda Mbezi beach ilianza.
Sio siri binadamu hawa walipendana na ndiyo maana muda wote walikuwa wenye furaha iliyozidi kiasi chake.
“Mama Kijacho”
Issa alianza utani baada ya kufika nyumbani.
“Karibu nyumbani baba kijacho”
“Ahsante Mke wangu”
Hapohapo Katrina bila kusita wala kusema kitu chochote kingine alimvuta Issa mdomoni mwake,akatoa ulimi wake akautumbukiza kinywani mwa Issa ukapokelewa vizuri wakaanza kunyonyana midomo kama makinda ya njiwa,damu zao zilianza kukimbia kwa kasi ya ajabu na kila mtu ilielekea alikuwa mwenye ugwadu na mwenzake ndiyo maana walianza kushikana huku na kule.Mkono wa Issa ulishuka taratibu mpaka kwenye sketi ya Katrina iliyokuwa na mpira akatumbukiza mkono wake ndani na kukumbana na chupi,akazidi kuudidimiza mkono wake chini zaidi ambapo huko alikutana na kitu anachokitafuta,Mgodi wa Katrina ulikuwa laini kama baga!
Hapo ndipo Issa alianza kuchezesha kidole chake akiwa anapima oil,mapigo ya moyo ya Katrina yalienda kwa kasi na alihisi kuishiwa nguvu za miguu mbali na hapo midadi ilimpanda ndiyo maana hata yeye akachukuwa mkono wake na kufungua akaupitisha tumboni mwa Issa akashuka mpaka chini na kufungua vifungo vya suruali akashusha zipu na kuingiza mkono wake laini ndani zaidi akakutana na gunzi lililotuna,nayeye akaanza kulichuwa taratibu.Mambo waliyokuwa yanafanywa yalikuwa mazito mno kwani nguo ya Juu ya Katrina ilitolewa na sidiria yake ikatupwa chini,kifua chake kikawa wazi.Kilichomfanya adhani wenda anapaa angani ni baada ya Issa kugusisha ulimi wake juu ya chuchu zake,hapo ndipo alipohisi kama anapaa angani na vitu anaviona kwa chini,mwenyewe akarudi kinyume nyume na kulala juu ya sofa kubwa,akaitoa sketi yake na kuchojoa chupi,akabaki kama alivyotoka kwenye tumbo la Mama yake.Hapohapo nayeye Issa akaanza kutoa nguo zake kwa haraka alimanusura shati lake ling’oke vifungo kutokana na haraka aliyokuwa nayo,akapanda juu ya sofa na kuchukuwa mguu mmoja wa kushoto wa Katrina na kuuweka begani kwake,akaseti ndizi yake vizuri na kuitumbukiza ndani ya mgodi wa Katrina ambao tayari ulikuwa na majimaji yanayoteleza!
“Aaaaaaaah sssshssss”
Kiuno cha Issa kilikuwa kinapanda juu na kurudi chini hiyo ilimfanya Katrina atoe sauti za puani na kwa namna ambavyo Issa alivyokuwa anazungusha kiuno chake ilimfanya apagawe zaidi na kufanya ahisi raha ambazo zilikuwa ngumu kuelezeka kiwepesi,tendo hilo lilidumu kwa dakika kadhaa lakini ilionekana hakuna mtu yeyote aliyetoshekwa ndiyo maana hata walivyofika chumbani mtanange ulizidi kuendelea sababu kila mtu alitaka kumridhisha mwenzake,kikubwa.Mechi hiyo ya ki utu uzima iliisha usiku wa saa sita kasoro mbili!
“Issa,nakupenda sana unajuwa”
“Hata mimi”
“Nihakikishie kuwa haitokuja kumvulia mwanamke yoyote yule nguo yako ya ndani”
“Nakuhaidi hilo”
“Una uhakika?”
“Ndio Mama Kijacho,nakupenda wewe tu”
Maneno hayo yalimfanya Katrina afarijike mno,akasogea karibu na Issa na kumlalia kifuani kwake.
“Mwanamke wako wa zamani alikuja hapa”
“Mwanamke wangu wa zamani?”
“Ndio”
“Yupi?”
“Marietha”
“Marietha?Alikuja hapa?Lini?Alikuwa anataka nini?”
“Anataka kuzungumza nawewe”
“Hapana siwezi”
“Baby kumbe Deo ni Mme wake?”
“Ndio ni mumewe”
Jibu hilo lilimfanya Katrina asogee nyuma kidogo na kumuangalia Issa bila kummaliza.
“Kumbe ulikuwa unajuwa?Kwanini ulinificha kitu kama hicho?Issa nini kinaendelea?Nambie ukweli”
Katrina alibadilika hapohapo na kutaka kujuwa mkasa mzima na maelezo yaliyonyooka kuhusu yeye na Deo!
*******
Marietha alijifananisha na mwanaharakati kwani alitaka kupambana mpaka dakika ya mwisho ahakikishe kuwa mumewe anatoka gerezani kwa namna yoyote ile ndiyo maana moyo wake ulijawa na kisasi kupitiliza.Hakuelewa njia gani atumie ili kumshawishi Issa amtoe Deo gerezani.
“Naamini Issa ananipenda bado,nitamuingia kwa gia ya kimapenzi.Ikifeli basi,lakini hapana kuna njia nyingine nyingi.LAZIMA NILIPE KISASI,HAWAWEZI KUISHI KWA FURAHA WAKATI MME WANGU YUPO GEREZANI”
Hiyo ndiyo mikakati iliyokuwa inapita kichwani kwa Marietha akitafakari jinsi ya kumkomboa mumewe gerezani,akiwa kitandani kwake usiku wa siku hiyo!



Ni kweli alidhamilia kumkomboa Mumewe gerezani kwa njia moja ama nyingine, ndiyo maana usiku mzima siku hiyo alikuwa akiwaza vitu vingi sana,kwa jinsi alivyomjua Issa nje ndani kwake kazi hiyo aliifananisha na kuweka tonge la ubwabwa mdomoni.
“Najua wapi udhaifu wake ulipo huyu mwanamme, hanipi shida yoyote ile.Nimekaa naye zaidi ya miaka nane,lazima Deo awe huru tu”
Marietha alihitimisha mawazo yake na zoezi lake aliliita ‘MAFIA SCOOP’ akatabasamu na kusubiri kukuche ili aanze kufanya mambo aliyopanga,kulivyopambazuka alikuwa wa kwanza kutoka kitandani,akaweka shuka vizuri akaingia bafuni akapiga mswaki na kujimwagia maji vizuri,akarudi kitandani ili avute mda mpaka ifike saa moja asubuhi kwani ndiyo kwanza ilikuwa saa kumi na moja ingawa alimsikia dada wa kazi anafagia nje lakini hakutaka kutoka kwanza,aliendelea kutafakari mpango wake wa kumuingia Issa mpenzi wake wa zamani kwa namna moja ama nyingine ili mradi Deo awe huru kwani kukaa gerezani kwa Deo kulisababisha maisha yake yayumbe mbali na hapo aliwaonea huruma sana watoto wake wadogo, ambao walihitaji malezi bora.
“Lazima nipambane mpaka mali za mume wangu zirudi hata kwa kumwaga damu ili namimi niende gerezani”
Hivyo ndivyo alivyowaza Marietha na bado aliendelea kuamini kuwa Issa alikula njama za kumfilisi Deo na alitafsiri jambo hilo moja kwa moja kama kisasi.

Ilivyotimu saa moja,akafungua mlango na kutokeza seblen hiyo ni baada ya kumsikia Mtui anaongea na huo ulikuwa muda wake wa kwenda kibaruani.
“Shemeji za asubuhi?Leo mbona mapema kiasi hicho?”
“Usingizi sina.Lakini nilikuwa nataka kutoka pia”
“Leo?”
“Ndio leo.Nataka kwenda kumsalimia rafiki yangu”
“Sawa,ngoja nikupe nauli kidogo”
Mtui hakuwa na kinyongo chochote sababu aliamini Marietha ni mtu mzima kwa hiyo hakuwa mwenye haja ya kumuhoji maswali ya juu ya wapi anaenda ama atarudi muda gani.Alichofanya yeye ni kuchomoa ‘wallet’ na kutoa elfu thelathini na kumkabidhi.
“Hiyo nyingine utaweka mfukoni,itakusaidia kufanya vitu vyako vya hapa na pale”
“Ahsante Shemeji”
Marietha alishukuru na kufurahi zaidi kwani aliamini kuwa kwa pesa hizo zingefanya mambo yake yawe rahisi mno.
Mtui alivyoondoka na kushuhudia gari limetoka nje ya geti yeye aliingia chumbani na kujiandaa harakaharaka kwa safari ya kwenda Mbezi beach kumsaka Issa pamoja na Katrina ili azungumze nao kwanza, hiyo aliita hatua namba moja na bado zilikuwa hatua nyingine mbili kwani jumla zilikuwa hatua tatu.
“Ya kwanza ikidunda,natumia namba mbili hiyo ikigoma.Itakuwa sina jinsi nitatumia namba tatu ya kumwaga damu”
Mpango mzima alikuwa nao kichwani na siku hiyo alijifananisha na FBI ama jasusi anayetaka kufanya ukombozi kwa Mateka.
Alivyohakikisha amejiandaa na kila kitu kipo sawa, alitoka nje na kuelekea kituoni ambapo huko alitafuta usafiri uliomshusha Ubungo,safari yake haikuishia hapo ilimlazimu apande daladala lingine la Mbezi,baada ya dakika kadhaa aliwasili daraja la Malesela na kushuka,akavuka barabara na kuanza kutembea kwa miguu mpaka alipofika nyumbani kwa Katrina, hapo ilikuwa tayari imejiri saa nne ya asubuhi,pembeni juu kidogo kulikuwa na kitufe cha kubonyeza kengele!Akakibinya.
“Ding dung”
Kelele ya kengele kutokea seblen zilipenya mpaka chumbani kwa Issa akiwa juu ya kiuno cha Katrina wakipeana raha za dunia,hiyo haikufanya asitishe zoezi lake kwani alikaribia kufika mshindo,alikadhalika kwa Katrina kwani isingekuwa rahisi kumruhusu Issa atoke juu ya kifua chake sababu hata yeye ndiyo alikuwa anafika mlima kitonga ndiyo maana alikuwa anamg’ang’ania!
“Ahh aaaah aaaah aaaaaaaaaaaah ssshss ssshsss aaaah”
Katrina alitoa sauti ya mguno na kuzidi kumvuta Issa karibu yake kabisa,raha alizohisi asubuhi hiyo ukichanganya na baridi lililokuwepo ilimfanya ahisi kuwa yupo juu ya bahari anaelea,hapohapo akafika mshindo na baada ya sekunde chache Issa akapasua yai la bata na kutulia juu ya kifua cha Katrina!
“Baby kuna mtu anagonga getini”
Katrina akasema baada ya kusikia kengele inalia tena kutokea seblen kumaanisha kuwa kuna mtu nje ya geti.
“Atakuwa nani asubuhi yote hii?”
“Mimi sijui”
“Asubuhi hii kuna mtu ulimwambia aje?”
“Hapana”
“Ngoja niende”
Issa alitoka kitandani na kuchukua kaptula bila kuvaa kitu chochote kile ndani,akatoka nje na kutembea mpaka getini.
Kabla ya kufungua mlango mdogo kwanza alifungua kidirisha kidogo ili ajuwe ni aina gani ya mgeni aliyefika asubuhi ya siku hiyo na anataka kitu gani.Macho yake yalikumbana na Marietha,mbali na hapo waligongana macho kwa macho.
“Issa nahitaji kuongea nawewe”
Marietha alizungumza harakaharaka bila nukta hiyo ni baada ya kumuona Issa kafungua kidirisha kidogo.
“Issa tafadhali nina shida sana”
“Nakusikiliza,ongea tu hapohapo”
“Issa usinifanyie hivyo wangu”
“Una shida gani Marietha?Nenda mke wangu akikukuta hapa haitoleta picha nzuri”
“Naomba niongee naye”
“Siwezi kukuruhusu”
Kwa Issa ilikuwa vigumu kufungua geti kwani kwa kufanya hivyo aliamini kuwa Katrina angegubikwa na wivu sababu alimjua sana mwanamke huyo wa Kihindi alivyokuwa mwenye wivu kuliko kawaida!

Kukaa ndani kwa zaidi ya dakika moja bila Issa kurudi chumbani kulimfanya Katrina atoke kitandani na kujitanda kanga mwili mzima akatokeza mpaka seblen na kunyoosha mlangoni,ambapo alisimama na kumuona Issa amesimama anazungumza na mtu lakini hakujua ni nani sababu alikuwa nje ya geti.
“Issa,ni nani huyo?”
Katrina akauliza, hiyo ilimfanya Issa apate kigugumizi kidogo.
“Marietha”
“Marietha?Anataka nini?”
“Sijui”
“Mwambie aingie”
Ruksa hiyo ilimfanya Issa afungue geti,Marietha akaingia ndani akiwa anashangaa huku na kule,akampita Issa na kunyoosha mpaka kwa Katrina.
“Za asubuhi?”
Akatoa salamu kwa sauti ya upole.
“Nzuri,una shida gani?”
“Nina mazungumzo nawewe”
“Nakusikiliza,unaweza ukasema hapahapa”
“Ni kuhusu mume wangu,anateseka sana kule Jela naomba ufanye uwezalo atoke”
“Yaani mimi nifanye nini?”
“Naomba umtoe nimezaa naye watoto wanapata shida sana”
“Mimi sina uwezo wa kumtoa subiri miaka kumi na tano ipite,isitoshe sisi hatuhusiki naomba ujue hilo.Wala hatuhusiki kabisa,kilichomfanya awe pale ni utapeli wake, kakutwa na pesa bandia.Hukuwa unajuwa kuwa mumeo anachapa pesa bandia?”
“Hapana Deo wangu hawezi kufanya kazi hiyo,namjua hajawahi kufanya kitu kama hiko”
“Aya sasa nikiamua kukusaidia na kwenda kukata rufaa,nitaenda kusema nini?”
“Kuwa yeye sio mwizi”
“Nitaanzia wapi?Sio mwizi kivipi wakati kakutwa na vithibiti?Dada haya mambo hayaendi kienyeji kama unavyofikiria,cha kukusaidia usubiri miaka kumi na tano hilo ndiyo suluisho”
“Na mali zake mlizomchukulia?”
Marietha hakuridhishwa hata kidogo na majibu aliyopewa na Katrina ndiyo maana aliendelea kurusha maswali tofauti tofauti ya hapa na pale kama askari,hiyo haikufanya Katrina achoke kumjibu.
“Mali zake zilichukuliwa na benki,wakapiga mnada tukalipwa pesa zetu tulizokuwa tunamdai.Ni hayo tu,una swali lingine?”
“Hapana unanidanganya”
“Kama huniamini,shauri yako.Na nachokuomba kitu kimoja sitaki kukuona hapa nyumbani kwangu tena.Kama unamtaka Issa kwa gia ya kujileta leta hapa,ukome tena ukome”
Katrina akabadilika ghafla na kuwa mkali kama pilipili, hiyo ilitokana na wivu uliomkaa kohoni tena ulimpanda ghafla hapohapo.
“Ondoka sasa hivi kwanza.Issa mtoe mwanamke wako,sitaki kumuona,alinikashfu sana”
Kila kilichokuwa kinasemwa na Katrina Issa alikisikia na amri aliyopewa pia,alichofanya ni kusogea mpaka kwa Marietha.
“Marietha samahani naomba uwende”
“Issa”
“Nenda tafadhali kama ulivyosikia na usitake nitumie nguvu sababu sitoshindwa”
“Issa kweli unaamua kunifanyia mimi hivi?”
“Nenda tafadhali”
Historia yao ilikuwa nzito kati yao, ndiyo maana Marietha alidiriki kusita kidogo kuondoka akimuangalia Issa machoni, hiyo ilifanya Issa akumbuke vitu vingi sana vilivyopita nyuma,akawa kama anaangalia mkanda wa kusisimua, akili yake ikamrudisha nyuma kwa kasi akajiona alivyokuwa na Marietha chumbani juu ya kitanda wanafanya ngono,akajiona anavyosaidiwa na kupewa pesa,akajiona jinsi alivyokuwa mwenye furaha kuliko kitu chochote kile.
Ghafla picha ya kanisani ikamjia na kumuona Marietha huyohuyo anafunga ndoa na Deo,akainuka na kutoka nje huko gari kubwa likamgonga akapoteza fahamu zake akasaidiwa na familia ya kihindi,Msichana mdogo aliyeitwa Katrina akampenda akamtunza na kumpa maisha mazuri,alivyokumbuka hayo tu akawa kama amezinduka kutoka usingizini!
“Marietha ondoka ondoka ondoka sasa hivi,toka toka toka tooooka”
Issa akafoka kwa ukali na kuanza kumburuza Marietha kumtoa nje!
“Issa,niachie”
“Nenda toka nje”
Akamvuta mpaka nje ya geti na kulifunga,kabaa!
“Nisikuone mahali hapa tena,shetani wewe”
Issa alikuwa amevurugwa kwa kiasi cha kutosha unyama aliofanyiwa na Marietha ulipita kichwani kwake hiyo ilifanya apandishe mori kama masai aliyepoteza shuka lake.
“Issa mimi nawewe tumetoka mbali.Kumbuka hilo”
Marietha aliropoka kutoka nje ya geti lakini hizo zilikuwa ni kama kelele za chura ambazo zisingeweza kumzuia tembo kunywa maji,akapitiliza Mpaka kwa Katrina.
“Issa unampenda Marietha?”
Akakumbana na swali kutoka kwa Katrina akiwa amevimba nayeye,wivu ulimjaa moyoni.
“Nakupenda wewe,hilo haliwezi kubadilika”
“Sio kweli”
“Kwanini unasema hivyo?”
“Kwanini ulisita kumtoa tangu mwanzo?”
“Katrina usiwe hivyo tafadhali”
Kama kawaida ya msichana huyu wa kihindi kuzila,hicho ndicho alichokifanya kwani aliingia ndani akiwa amebenua mdomo hilo halikumsumbua Issa sababu alijuwa tabia za mpenzi wake,nayeye akamfuata nyuma nyuma wakaingia wote mpaka chumbani.
“Katrina,What is wrong with you my love?”(Katrina, una tatizo gani mpenzi)
“Nothing”(Sio kitu)
“Try to control your emotions”
Kibarua kingine kikazuka siku hiyo cha kumtuliza Katrina na Issa alijitahidi kumuimbisha akijaribu kutumia njia nyingi tofauti tofauti lakini wapi,mtoto huyu hakucheka na isitoshe siku hiyo hakula kabisa mawazo yake yalimtuma kuwa ipo siku moja Issa atamsaliti na ndiyo maana hakuwa hata mwenye mudi ya kufanya kitu chochote kile,akaenda seblen mwenyewe akiwa anatafakari vitu vingi sana kichwani mwake!Kifupi siku yake ilivurugika.
“Katrina leo nitakupikia,ushawahi kula biliani wewe?Ubwabwa wa rangi”
Issa akatokeza seblen akiwa na mwiko anajaribu kutumia gia nyingine kumuingia Katrina.
“Sina Njaaa”
“Mmmh”
Issa akasogea taratibu mpaka kwa Katrina akaanza kumtania na kumtekenya, hapohapo Katrina akaanza kucheza wakaanza kurushiana mito yaani ‘pillow fight’hawakutofautishwa na watoto wadogo,wakavutana na kuanza kunyonyana ndimi zao kwa fujo yaani wakaanza kupigana madenda!
“Nakupenda sana Issa,nina wivu mno”
“Nalijua hilo,siku hizi hunipi shida”
“Kwenda huko ndiyo maana unafanya makusudi”
“Sio makusudi”
“Ijumaa naomba iwe siku ya ndoa yetu”
“Leo ni lini?”
“Jumanne”
“Aya mpenzi”
Katrina hakuchelewa jambo la Marietha kuonekana kwake kila wakati lilimtia mashaka sana na ilikuwa chachu ya kumfanya atake ndoa harakaharaka ili awe mke wa Issa,ndiyo maana dakika hiyohiyo akainua simu yake na kumtafuta Mama yake mzazi ili aanze kufanya taratibu za harusi siku ya Ijumaa,akamtafuta pia Kishipa na chogo ili awapashe habari, hawa walikuwa marafiki wakubwa sana wa Issa.
“Kuna kadi ishirini double kwahiyo nataka watu arobaini bure Chogo…Ndio ndio..Issa anaendelea vizuri yupo hapa…Yuko mbali kidogo lakini sawa..Ah ah nishaongea na Kishipa tayari,hahahaha acha utani basi..Msosi upo wa kutosha bwana,nawewe kwa kula..Aya sawa ahsante sana”
Kutokana na dunia kuwa kama kijiji na Teknolojia kukuwa ilifanya habari hiyo isambae kwa kasi ya upepo usiku huohuo!

Shamrashamra zikaanza kuanzia siku iliyofuata na haikujulikana habari za Issa kufunga ndoa zilimfikiaje Marietha lakini alizipata,hakutaka kuamini sababu alichukulia kama ni uvumi tu, akafunga safari mpaka Mbezi beach ili kuhakikisha,kazi yake ikawa ni kudadisi.Moyo ulimuuma kupita kiasi na wakati mwingine alitamani yeye ndiye aolewe kifupi alihisi anampenda Issa,mbali na hapo Issa alikuwa ni mwanamme aliyemuonesha usichana wake,akamfundisha mapenzi.
“Hii ndoa haiwezi kufungwa”
Marietha aliapia akiwa ndani ya daladala njiani anarudi,alivyokumbuka kuwa Mtui ana bastola akapata wazo jipya hapohapo.
“Lazima afe mtu siku hiyo.Haki ya Mungu tena”Aliapia!
Ni kweli alivyofika nyumbani siku hiyo hakulala mapema,alikuwa akimsubiri Mtui kwa hamu kubwa sana,mpaka inafika saa tatu Mtui hakutokea lakini hakuvunjika moyo,aliendelea kusubiri.Saa nne kasoro gari lilipiga honi akakaa vizuri,akasikia muungurumo wa gari.
“Shemeji bado hujalala?”
Mtui akaanza kutoa salam.
“Nipo macho kuna tamthilia nafuatilia hapa”
“Aya bwana,mimi nimechoka kweli leo nilikuwa kwenye kikao cha harusi”
“Pole na uchovu”
“Shem”
Marietha akaita baada ya kumuona Mtui anataka kukatiza kordo ili aingie chumbani kwake,akasimama.
“Nina shida nawewe”
“Shida gani hiyo?”
“Kuna kitu nataka unifundishe”
“Kitu gani?”
“Naomba nifundishe kitu kimoja hivi”
“Kitu gani?”
“Kutumia silaha yako”
“Silaha yangu?”
“Ndio”
“Bastola?”
“Ndio”
Mtui aliganda kidogo na kumuangalia Marietha kwani jambo hilo hakutarajia kulisikia kutoka kwa mwanamke huyu,Marietha!



Ni kweli hakutania kwani alitaka kujuwa kutumia silaha ya moto na akishafahamu akafanye uvamizi kwa kumuuwa Katrina na Issa kisha yeye ajipige risasi afe hapohapo,ilikuwa ni bora wakose wote.Hakuelewa kuwa pepo baya la umauti ndilo lililomvaa na kumpeleka puta,nyuma ya kisasi hiko kilitokana na wivu aliokuwa nao ingawa hakuelewa ni kwanini moyo wake unaumia kwani biashara yake na Issa ilishaisha siku nyingi mbali na hapo alikuwa mke wa mtu tayari.Akiwa seblen aliendelea kumsihi Mtui amuelekeze jinsi ya kutumia bastola.
“Kwanini?”
Mtui akauliza,alitaka kujua sababu.
“Nataka tu nijue shemeji hata hivyo nataka kwenda jeshini baadaye baadaye hivi”
“Bastola ni hatari ujue”
“Naelewa shemeji,naomba nifundishe tu kuitumia”
“Basi Jumamosi nikirudi kazini”
“Ningependa kujua leo”
“Sasa hivi?”
“Ndio”
Marietha alikuwa kama ruba siku hiyo kwani alimganda Mtui kupita kiasi,akazidi kumlazimisha jambo analotaka liwe tena usiku huohuo.
“Basi ngoja nikabadili nguo”
Hatimaye Mtui akakubali bila kujua kichwani kwa Marietha kuna mipango kabambe na endapo angemfundisha si ajabu nayeye angewekwa ndani kwani Marietha alitaka kutumia pia silaha ya Mtui kufanya mauaji.
Baada ya dakika tano Mtui akatoka akiwa na bastola mkononi yaani mguu wa kuku kwa Kiswahili cha geto!
“Kwahiyo kweli unataka kujua kutumia bastola?”
Mtui akauliza tena,bado swala la Marietha halikumuingia akilini hata kidogo.
“Ndio,naomba niishike”
“Subiri kidogo”
“Kacha kacha”
Mtui akakoki bastola niya yake ilikuwa ni kutoa risasi iliyoingia ndani ya chemba kwani bastola ukikoki risasi inapanda juu na ukikoki tena ni lazima risasi idondoke chini,hiyo ndiyo ilikuwa niya ya Mtui na baada ya hapo akachomoa magazine iliyokuwa na risasi kisha kumkabidhi Marietha bastola ambayo haina kitu ndani.
“Eh,kumbe nzito nzito hivi”
Marietha akasema baada ya kuiweka mkononi mwake.
“Nzito ndio”
“Sasa hapa ukitaka kumfyatua mtu unafanya nini?”
“Kwanza unaangalia hapo chini kwenye safety,kuna lock hapo.Una hakikisha hicho kidude kinakuwa unlock,unakoki bastola”
“Unakoki?Kukoki ndiyo nini?”
Siku hiyo Mtui hakutofautishwa na mwalimu wa darasani,akaanza kutoa kisomo kwa Marietha jinsi ya kutumia bastola akamfundisha pia jinsi ya kushika na kulenga shabaha!
“Mfano kama mtu yupo Mbali na unataka kumlenga,unaweka bastola hapa.Unashika na mikono miwili.Usipokaza mikono inakurudisha nyuma”
“Embu weka risasi tujaribu”
“Hapana,sio hapa”
“Shemeji wewe ushawahi kuuwa mtu?”
“Ndio”
“Ilikuwaje?”
“Ilikuwa huko Njiro Arusha usiku,naendesha gari.Mvua siku hiyo ilikuwa inanyesha sana barabara mbovu.Nikawa napita pori kwa pori kufika njiani nikakuta Wanaume wanne wamemteka mwanamke wanamuibia na wanataka kumbaka,nikapiga risasi hewani kumbe mmoja kati yao alikuwa ana bastola.Basi ndiyo mambo yakaanzia hapo”
“Ulifanikiwa kuwauwa wote?”
“Niliuwa wawili,mmoja nilimjeruhi”
“Wewe je?”
“Nilipigwa risasi moja ya mkono”
“Pole sana”
Siku hiyo Marietha alimchimba sana Mtui na kutaka kujua vingine zaidi,mpaka anaingia kulala alishajua kidogo kuishika.
Kitu kilichomjia mbele yake ni kuuwa tu lakini kwa kufanya hivyo peke yake angeishia gerezani hivyo alibadili mawazo pia na kutaka kujiua nayeye kwani asingeweza kukubali ahukumiwe.Usiku kucha aliwaza vitu chungu mzima na mara nyingi picha akiwa na Issa ilimpitia,akajiona walivyokuwa kitandani anaridhishwa vizuri na mwanaume huyo ambaye alijuwa kukata kiu yake vilivyo,alimuonea wivu sana Katrina kwa namna ambavyo anavyofaidi utamu wa Issa kitandani.
“Lazima kwanza nimuuwe yule kibiritingoma wa kihindi.Lazima aniachie Issa wangu.Deo nisamehee mume wangu”
Hakuwa Marietha bali ni wivu na hasira ndivyo viliyomsukuma na kumpelekea atake kumuuwa Katrina akiamini kuwa ndiye aliyemchukua Issa wake, kwa akili fupi aliyokuwa nayo hakuwaza kwamba yeye ndiye alikuwa mkandarasi wa kila kitu kutokea.

Asubuhi kulivyokucha akaonana na Mtui na kumkumbusha ahadi yao ya kuwa wanaenda misitu ya Changanyikeni ili kumfundisha jinsi ya kutumia bastola.
“Leo nitarudi mapema”
“Sawa nitakusubiri”
“Kwanini unataka kujuwa kutumia silaha?”
Mtui akauliza, kuna jambo alianza kulihisi lisilokuwa la kawaida.
“Nataka tu kujuwa shemeji”
“Isije ikawa unataka kuvamia”
“Ha! Haa! Haaa! Haaaa! Siwezi nitaanzia wapi?”
Marietha akajichekesha lakini ukweli wa kila kitu alikuwa nao moyoni mwake.
*******
Kama Mtui alivyohaidi ndivyo ilivyokuwa kwani mchana wa saa saba alirudi nyumbani kwake akala kisha kuondoka na Marietha mpaka katikati ya msitu uliokuwa Changanyikeni,waliamini huko hakuna mtu yoyote yule hivyo walitaka kutumia sehemu hiyo kufyatua risasi mbili ingawa Mtui alijuwa anaenda kinyume na sheria kwani kuna sehemu maalum za kufanya jaribio hilo la kulenga shabaha.Alichofanya ni kuchomoa ‘magazine’ na kupukutisha risasi kumi,zikabaki mbili.
“Hizi ndizo tutatumia kwa siku ya leo.Tutakuja wakati mwingine hapa si salama tutashtakiwa.Moja nitaipiga mimi utaangalia ninavyofanya kisha nyingine nitakupa”
“Sawa”
Marietha aliitikia kwa umakini lakini alikuwa mwenye uwoga fulani kwani katika maisha yake hakuwahi kufanya jambo kama hilo,ndiyo maana alikuwa mwenye hofu kuliko kawaida!
“Unaona ninavyoshika bastola,unakoki kama hivi.Sasa hapa chemba ipo wazi,ukivuta triga risasi inachomoka kuwa makini na unavyolenga.Unashika kwa mikono miwili namna hii”
Mtui alizungumza kwa vitendo,kila alichoongea kilishahabiana na vitendo, alivyokamata bastola kwa mikono miwili akabana jicho moja kidogo,akavuta triga.
“Paaaaaaa”
Mlio wa bastola ukasikika risasi ikachomoka na kupiga mti,Ndege waliokuwa porini wote wakapukutika na kuanza kuruka huku na kule,Mlio huo ulifanya mapigo ya Marietha yapige kwa nguvu maana ulikuwa ni mkubwa mno na wa kuogopesha jambo ambalo hakulitegemea hata kidogo hiyo ilifanya mpaka aanze kuogopa.
“Kamata,njoo upige.Imebaki risasi moja peke yake”
Marietha alishika bastola huku akitetemeka kupita kiasi,alimuangalia Mtui mara mbilimbili akawa kama mtu asiyeamini.
“Usitetemeke kama haupo tayari,tufanye siku nyingine”
“Hapana naweza kufyatua”
“Angalia vizuri mbele,vuta hiyo triga hakikisha unakaza mikono”
“Sawa”
Jasho jingi lilimtoka na akaanza kuhesabu kuanzia moja mpaka tatu.
“Paaaaaa”
Badala ya kupiga mti bastola ikaenda juu sababu hakukaza mikono, hiyo ilimfanya aogope zaidi na kuitupa pembeni na kama kungekuwa na risasi nyingine ndani lingekuwa jambo lingine.
Kufumba na kufumbua mwili ulikuwa umelowa jasho hiyo yote ni kwasababu ya hofu iliyomtanda.
“Umeumia?”
Mtui aliuliza baada ya kuokota bastola yake chini,akarudisha risasi na kumuinua akaanza kuondoka naye kuhofia watu ama askari kufika eneo hilo na kuhoji maswali.Waliingia ndani ya gari na safari ya kurudi nyumbani kuanza mara moja huku Marietha akiwa bado anatetemeka na pia anawaza jinsi atakavyofyatua risasi na kumuuwa Katrina pamoja na Issa na mwisho kujimaliza mwenyewe,alivyowakumbuka watoto wake alihisi moyo kumuuma!
*********
Shamra shamra zikiambatana na amsha amsha zilizidi kuendelea na simu zilikuwa zinaruka huku na kule,kila mtu alipashwa habari juu ya harusi ya Issa na Katrina.Mambo yaliandaliwa harakaharaka na baada ya siku mbili kila mtu alikuwa ana taarifa juu ya harusi hiyo iliyopanga kufanyika Kwalalumpa huko Sinza kwa Lemi,ulikuwa ni ukumbi mkubwa na wa kisasa wenye uwezo wa kuchukuwa watu zaidi ya elfu moja.Harusi iliandaliwa kwa umakini na mpaka vikao vinaisha kamati iliweza kukusanya shilingi milioni mia moja za kitanzania,matajiri mbali mbali walichangia, licha ya hayo Dokta Khaila alitoa shilingi milioni sabini taslimu kama mchango.
Mambo yalienda mbio mbio kuliko kawaida na Katrina alionekana akiwa mwenye mushkeli na alitamani siku zisogee mbele chap chap ingawa zilibaki siku tatu ili siku ambayo ingekuwa ya kihistoria kwake itimie kwani kuolewa na Issa kwake ilikuwa ni ndoto na ilikuwa lazima itimie.
“Baby basi lala nawewe”
“Sina usingizi hata kidogo”
Katrina alijibu wakiwa chumbani,hakujisikia kulala, muda wote alikuwa anawaza harusi na siku zilizobaki kwake alizifananisha na mwaka.
“Una mcheche”
“Lazima niwe nao baby.Alafu hoteli ile kuna vitu pia vitaagizwa kutoka China”
“Ushaongea na Rhoda Denis?”
“Ndio”
“Good”(Vizuri)
Hayo ndiyo mambo yaliyokuwa yanaendelea kwa wanandoa hawa watarajiwa!
*******
Marietha bado hakukata tamaa baada ya kujifunza kutumia silaha alianza kufanya upelelezi wake chini kwa chini,baada ya siku mbili alipewa nyepe kuhusiana na ukumbi ambao Issa na Katrina wangefunga ndoa,siku hiyohiyo baada ya kujuwa akatafuta usafiri na kupelekwa Sinza nje ya ukumbi wa Kwalalumpa.
“Kaka hapa ndio kwalalumpa?”
Marietha akamuuliza kijana mmoja aliyekuwa anapita kandokando ya barabara.
“Ndio sista,ukumbi ndiyo huo.Ni mzuri sana unataka kukodi?Chukua namba zangu”
Kijana alidhani amepata bingo na niya yake ilikuwa ni kujifanya dalali ili apige pesa lakini kwa Marietha hakuhitaji kukodi ukumbi bali alitaka kuua watu siku ya Ijumaa.
Aliondoka na kurudi nyumbani harakaharaka ili kupanga mikakati ya jinsi ya kuvamia na namna ambavyo angechukua bastola ya Mtui bila yeye kugundua.Kila siku alitafakari usiku na mchana!
********
Siku ya siku ilifika na Ijumaa ndiyo ikawa imewadia, siku ambayo Marietha alitaka kuuwa, mapigo yake ya moyo yalikuwa yakipiga kwa kasi ya ajabu,alijua jambo analoenda kulifanya lilikuwa ni hatari lakini hakutaka kurudisha moyo wake nyuma.
“Nishaamua tayari sipo tayari kuwaacha wale wanyama waishi bora wote tukose”
Marietha alitafakari siku hiyo mchana akiwa peke yake.Na siku zote Mtui huwa anawahi kurudi siku za Ijumaa,aliamini kuwa ndiyo ungekuwa muda muafaka kwake kuiba silaha ya Mtui kisha kwenda kuuwa.
Ni kweli ilivyofika saa kumi na mbili kasoro jioni,gari la Mtui liliingia ndani, wakasalimiana na Mtui akaingia chumbani.Hapohapo akanyata taratibu mpaka mlangoni kwa Mtui,akatega sikio,alivyosikia maji yanamwagika bafuni akasukuma mlango na kuingia ndani ya chumba akiwa anatetemeka, hakuelewa angesema nini endapo Mtui angetoka bafuni na kumkuta chumbani kwake,alijuwa vizuri sana kwamba bastola itakuwa chumbani sababu Mtui asingeweza kuingia nayo bafuni kuoga nayo.Akakifikia kitanda na kuanza kutupa nguo huku na kule bila mafanikio,akatembea taratibu mpaka kwenye kabati na kuvuta droo lakini wapi!
Jasho likaanza kumtoka,akarudi tena kitandani na kuvuta mto,moyo wake ukapiga paa!Alikuwa tayari ameiona bastola, jasho likazidi kumtoka zaidi,akaibeba na kutoka nayo nje harakaharaka, akaingia chumbani kwake bila breki akaiweka ndani ya mkoba,bila kuaga anaenda wapi akatoka nje ya geti.
“Psii pssiiiii.Boda boda”
Marietha akaita,siku hiyo aliamua kupanda pikipiki ingawa alikuwa ni muoga kupita kiasi.
“Nipeleke Sinza kwa Lemi, Kwalalumpa Hall”
“Kumi na tano hapo”
“Poa”
Hakukuwa na haja ya kushushana bei ingawa alijua dereva wa bodaboda kataja pesa ndefu.Si anaenda kujiua?Aanze kushusha bei kwanini yaani!Marietha siku hiyo alikuwa kama Nabii, sababu alikiona kifo chake.
“Kaka fanya haraka nikichelewa sitokupa pesa yako”
“Poa poa sista”
Pikipiki ikapigwa gia,niya ya Marietha ilikuwa kuwahi kabla ya Issa na Katrina kuingia ndani ya ukumbi ili awapige risasi palepale nje ya ukumbi kisha nayeye ajiue!
Ni kweli,ndani ya dakika ishirini waliingia Sinza kupitia njia za panya,hatimaye wakaibuka Sinza katika ukumbi wa Kwalalumpa.
Akaingiza mkono ndani ya mkoba wake na kutoa pesa!Akampa dereva ujira wake,akatembea mpaka kandokando akiangalia kama bibi na bwana harusi wameingia.

Shamrashamra na hekaheka alizozikuta zilimshangaza,kulikuwa na magari mengi sana ya kifahari.Katika kuchunguza kwake aligundua kuwa maharusi bado hawajawasili lakini wanakaribia kufika,moyo wake ulizidi kupiga kwa kasi kwa kitendo ambacho angeenda kukifanya muda mchache ujao.
“Piii piii piii..Pipipiiiiiiii..Pii piiiiiiii”
Kushoto kwake kulikuwa na magari yanayotembea kwa mtindo wa msululu yakiwa yamewasha taa na katikati ya msafara huo kulikuwa na gari refu jeusi la milango sita yaani ‘limonzine’ gari zinazofanana na benzi lakini ni ndefu mno kwenda nyuma,lilikuwa ni jibu tosha kuwa Issa na Katrina wapo ndani ya gari hilo.Huo ndio ulikuwa muda wake muafaka wa kufanya mauaji,akaanza kusogea karibu zaidi huku akiingiza mkono mmoja ndani ya mkoba.
“Bwana harusi kapendeza sana Duuu…Issaaaaaaaaa”
Kelele za mtu aliyekuwa pembeni ndizo alizosikia baada ya Issa kuteremka kutoka ndani ya gari,akamsubiri mpaka Katrina ashuke,akawashuhudia wameshikana mikono kwa ajili ya kuingia ndani ukumbini,kulikuwa na umati sana wa watu.
“Hapa hapa”
Marietha hapohapo akachomoa bastola kutoka ndani ya mkoba wake.
“Kacha kacha”
Akaikoki,kila mtu alishtuka na wengine wakaanza kurudi nyuma.
“Issa..Siwezi kuendelea kukuona ukiwa una furaha wakati mme wangu yupo gerezani.Hapana,leo nakuuwa”
Ni Marietha ndiye alikuwa anaongea huku bastola ikiwa mikononi mwake,kidole taratibu kinarudi nyuma anavuta triga.
“Paaaaaaaaaa”
Ni mlio mkubwa ndio uliosikika,damu ziliruka na risasi ilipenya katikati ya kifua cha Issa ikatokea upande wa pili,wageni waalikwa wote walisambaa na wengine walizimia kutokana na mlio mkubwa.
“Paaaaaaaa”
Ni risasi nyingine iliyotoka na kupenya ndani ya kichwa cha Katrina akadondoka chini.Damu zilikuwa zimezagaa chini bila kupoteza wakati,akajiwekea bastola kichwani ili ajiftyatue ajiue!


Jasho lilikuwa linamtoka mwili mzima na alikuwa anaweweseka kitandani kuliko kawaida,hapohapo alikurupuka kutoka kitandani akasimama kama mtu aliyechanganyikiwa na kutoka kitandani kama mwanajeshi aliyeshtuliwa lindoni na mkuu wake wa kazi,akaparamia ukuta na kubonyeza ‘Switch’ ya taa.Ni ndoto mbaya aliyoota amempiga risasi Issa na Katrina, ndiyo iliyofanya mpaka mapigo yake ya moyo yapige mpaka kutaka kutokeza nje ya kifua chake,kitanda chake kilijaa jasho jingi kupita kiasi.Anahema juujuu.Ndoto aliyoota ilizidi kumpitia kichwani hiyo ni kutokana na hofu aliyokuwa nayo moyoni.
“Mungu wangu”
Alisema huku akihema juu juu,Marietha alirudi kitandani kulala lakini kitu usingizi kilikuwa hadimu sana kupatikana baada ya kuota ndoto hiyo.
Kulivyokucha hakutoka kitandani alikuwa akitafakari bado jinsi ya kuiba bastola ya Mtui ili akafanye mauaji baada ya siku moja kupita.Ingawa aliota lakini hakutaka kurudisha moyo wake nyuma, ilikuwa ni lazima amuuwe Issa na Katrina ukumbini na baada ya hapo nayeye ajipige risasi afe.Kitu kilichomtatiza ni namna ambavyo angeiba bastola ya Mtui.Alihisi mwili wake unamtetemeka kupita kiasi kwa kitendo ambacho angeenda kukifanya,Marietha hakuwahi kuuwa ama kuwaza kama atakuja kuuwa mtu mbali na hapo aliamini kuwa mapenzi yana nguvu kupita kiasi,aliwahi kusikia watu wanajinyonga na kuwaona wajinga na wapumbavu.
“Lazima niue,acha namimi nionekane mjinga na mpumbavu”
Hivyo ndivyo alivyowaza Marietha, akijaribu kuvuta picha jinsi alivyokuwa ndotoni.Ilikuwa bado ni alfajiri na mapema na hiyo ndiyo ilikuwa mida ya Mtui kujiandaa na kwenda kibaruani,akasubiri mpaka alivyohisi ameondoka kwa kuhakikisha hilo akafungua pazia la chumbani kwake na kuliona jinsi gari linavyotoka nje ya geti!Hapohapo akatoka kitandani na kufungua mlango wake.
“Dada”
Akaita.
“Abee”
“Naomba kaninunulie sabuni ya Unga dukani,nataka nije kufua nguo zangu”
“Weka tu hapo nitakusaidia kuzifua”
“Hapana usijali,kaninunulie nitazifua mwenyewe.Shika hii pesa”
Marietha hakuwa mwenye niya ya kufua bali ni kumzuga dada wa ndani atoke nje ya geti kisha yeye azame chumbani kwa Mtui aangalie bastola kama ipo ingawa hakuelewa angeifanyia nini kwa wakati huo kama angeikuta,hicho ndicho kilichotokea kwani baada ya dada wa ndani kutoka nje yeye aliingia kwa haraka chumbani kwa Mtui na kuanza kukagua huku na kule.
Alionekana yu mwenye hofu sana kwani angeshindwa kujibu swali la Mtui endapo angemkuta ndani ya chumba chake ndiyo maana alikuwa akitafuta huku na kule kwa haraka tena kwa staili ya kurusha rusha mito,akaingia mpaka kwenye madroo akayavuta, huko alikumbana na maboxi yaliyojaa risasi.
“Itakuwa wapi?Kaondoka nayo huyu”
Haikuwezekana hata kidogo kwa Mtui kuondoka na kuiacha bastola yake nyuma, hilo lilikuwa wazi kabisa kwani aliinunua ili atembee nayo na sio kuiacha chumbani.Baada ya Marietha kujiwa na wazo hilo alirudisha vitu kama vilivyokuwa na kutoka nje ya chumba na kuingia chumbani kwake ambapo huko alizidi kupanga mikakati kabambe ya kufanya mauaji ya kikatili siku ya ndoa ya Issa na Katrina!
“Itakuwa Mungu kanionesha njia ya kuiba bastola”
Aliwaza Marietha baada ya kuikumbuka ndoto yake.Aliamini kwamba Mungu alimuotesha ndoto hiyo kwa makusudi hivyo ilikuwa ni lazima auvae ujasiri na kujaribu.Moyo wake ulizidi kutapatapa na alitakiwa kutumia fomula ya kuingia chumbani kwa Mtui akiwa anaoga kama alivyooneshwa ndotoni jambo ambalo lilikuwa gumu sana kwake,kilichomfanya azidi kuchanganyikiwa ni kwa namna ambavyo masaa yalivyokuwa yanakimbia kwa kasi ya risasi.
Ilikuwa ni siku ya Alhamis saa nane mchana kumaanisha kuwa ana masaa yasiyopungua ishirini na sita,hapo ndipo taa yake nyekundu ilianza kuwaka kichwani kuwa afanye mambo himahima!
**********
Wakati Marietha anawaza kuwauwa, wao walikuwa na furaha isiyokuwa na kifani,ndugu jamaa na marafiki walipashwa habari juu ya harusi hiyo kubwa ambayo walihisi ingeenda kuzungumziwa na watu wengi na kutingisha jiji la Dar es salaam kwa ujumla, ndiyo maana Katrina alitafuta pesa nyingi sana ili kufanya harusi yake iwe ya kimataifa.
Kwao siku zilikuwa zinaenda taratibu sana.
“Baby sipati picha hiyo Ijumaa itakuwaje?”
Katrina ndiye alikuwa anauliza akiwa kifuani mwa Issa macho yamelegea,hana nguo hata moja wamejifunika shuka moja kumaanisha kuwa muda mfupi walitoka kufanya ngono.
“Itakuwa kama kawaida”
“Nimetafuta walinzi”
“Walinzi wa nini?”
“Baby umesahau kilichotokea,sitaki tena kosa lile lile lijirudie”
“Haina haja love”
“Lakini baby…”
“No haina haja,walinzi wa mlangoni wale watatosha tu”
“Okay mpenzi wangu.Nakupenda sana,huyu mtoto wetu akizaliwa tumuite nani?”
“Mama kijacho,hata miezi miwili bado hajafikisha!”
“Sasa si naanza mikakati kabisa”
“Sawa nitafikiria”
“Okay baby”
Siku hiyo waliongea mengi sana na siku zote kila mtu alimuona mwenzake mpya kwani baada ya hapo walianza kuchokozana kwa kushikana na mwishowe wakaingia katika dimbwi la raha,kutokana na furaha waliyokuwa nayo kila mtu siku hiyo alitaka kumburudisha mwenzake kwa jinsi anavyojua yeye,ilikuwa mara Katrina akae kwa juu,mara ashike kona ya kitanda na baada ya sekunde tano akalala chali yaani kifo cha mende hapo ndipo alipofika mshindo,Issa akabaki juu ya kifua jasho linamtoka kwa mbali.
“I love you so much”(Nakupenda sana)

*******

Vitu vingi sana vilipita nyuma,bado alimuwaza Issa na alihisi kumpenda bado lakini hakuelewa ni kwanini ghafla namna hiyo kwani alikuwa tayari ni mke wa mtu na badala ya kusikitika na kutafakari juu ya mateso anayopata Mumewe Deo gerezani yeye alikuwa anamuwaza Issa Nurdin Mpelembe!
“Siwezi kukuacha Issa,lazima tufe wote”Aliapia.
Masaa,dakika na sekunde vilisogea kwa haraka hatimaye siku ya Ijumaa ikawadia.
Siku hiyo Marietha alikuwa mpole na alimuomba Mungu wake msamahaa kwani alijua anaenda kuuwa na kufa.
“Nisamehee Deo nisamehee wanangu.Buliani”
Hivyo ndivyo alikuwa akitamka Marietha huku machozi yakimlenga.Fununu alizopata kuhusu ukumbi zilifanya achore ramani kichwani jinsi atakavyoingia ukumbi wa Kwalalumpa na kufanya mauaji hayo kisha nayeye kujipiga risasi na kufa hapohapo.
Aliamini ulikuwa ni unyama lakini hakujali hilo,siku hiyo aliisubiri mpaka Mtui arejee kutoka kazini na siku za Ijumaa huwa ana kawaida ya kurudi mapema ndiyo maana alimsubiri kwa wudi na uvumba!
Moyo ulizidi kupiga kwa nguvu ilivyotimu saa kumi na moja jioni, hasahasa alivyosikia honi ya gari kutokea kwenye geti,kwake jioni ilikuwa ni muda wa maangamizi!Mtui akaingia ndani na kukaa kwenye kiti badala ya kuingia moja kwa moja chumbani kama anavyofanya kila siku.
“Shemeji vipi?Mbona hukai?”
Mtui alihoji baada ya kumuona Marietha amesimama ukutani.
“Hapana,nipo tu.Nimechoka kukaa tangu asubuhi nimeshinda nimelala”
“Ngoja nipumzike kidogo hapa”
Kauli hiyo kutoka kwa Mtui ilimkera sana Marietha kwani alikuwa na mipango yake,ilikuwa ni lazima Mtui aingie chumbani kwake kujimwagia maji ndipo hapo Marietha atumie mwanya huo kuiba silaha!Uhakika wa Mtui kuwa na bastola alikuwa nao sababu aliona kiuno chake upande wa kulia kuna kitu kimevimba hiyo ilitosha kabisa kuamini kuwa ilikuwa ni bastola.
“Leo hutoki?”
Uzalendo ulimshinda, akauliza.
“Mimi?Leo nipo seblen hapa kwanza nitatoka usiku kidogo.Vipi kwani?”
“Nauliza tu maana sio kawaida yako Ijumaa kama leo kukaa seblen”
“Ni kweli,najinyoosha tu hapa kisha niingie chumbani”
“Basi aya,mimi naingia chumbani”
“Sawa”
Kama Mtui angeendelea kubaki Seblen basi mipango ya Marietha ingeenda kugonga mwamba jambo ambalo hakutaka litokee, alitamani amfuate Mtui amwambie anahitaji Bastola yake lakini aliamini angeharibu operesheni nzima ambayo aliipanga siku nyingi sana zilizopita.
Kazi yake ilikuwa ni kuzunguka huku na kule akitafakari jinsi ya kufanya akiwa chumbani,alivyotupa macho yake juu ya saa kubwa ilikuwa kumi na moja kasoro hapo ndipo alipochanganyikiwa zaidi.Ghafla akahisi mlango wa chumba cha Mtui umefungwa,akasimama na kutembea kwa hatua chache na kunyonga kitasa akatoka kwenye kordo na kuchungulia Seblen,Mtui hakuwepo.
Moyo wake ukapiga kwa nguvu akatembea kwa hatua za taratibu mpaka mlangoni kwa Mtui,akatega sikio lake!
“Ngoja nikaoge basi nakuja sasa hivi,ndio ndio.Mimi nakunywa Heinken leo au Ndovu,yes yes.Okay okay,nikianza kutoka nitakwambia.Shukrani”
Maongezi kupitia simu akiwa ndani chumbani yalitoka mpaka nje kwa Marietha aliyetega sikio lake moja mlangoni,shabaha yake ilikuwa ni Mtui kuingia bafuni kuoga kisha yeye aingie ndani chumbani akwapue bastola na kukimbia mbali,hiyo ndiyo ilikuwa mipango yake kichwani.Aliendelea kutega sikio, akasikia maji yanamwagika kutokea bafuni hiyo ilimaanisha Mtui kwa wakati huo anaoga,akanyonga kitasa kikafunguka moyo wake ukapiga paa!Baada ya kuingia ndani,akanyata kidogo mpaka kitandani kabisa akatoa shuka,akatizama huku na kule huku akiwa mwenye hofu kupita kiasi.
“Griii griiiii,Griii griiiii”
Marietha alihaha sababu simu ya Mtui ilianza kuita tena kwa sauti, kivyovyote vile Mtui angetoka bafuni na kuipokea,alikuwa ni kama ametabiri kwani maji yaliyokuwa yanamwagika kutoka bafuni yalikata kumaanisha kuwa Mtui kafunga bomba.Akili ya Marietha ikafanya kazi kwa kasi ya umeme,mlango ulikuwa mbali na asingeweza kuufikia na kutoka nje kabla ya kukutwa, ilikuwa ni lazima ajifiche! Kwa haraka akakimbia mpaka kwenye pazia na kukaa nyuma!Jasho linamtoka, Mtui akatoka bafuni kama alivyo hajavaa nguo hata moja mwilini mwake,ndizi yake kubwa inaning’inia Marietha alihisi kutetemeka sababu hakuwahi kumuona Mtui akiwa kama alivyozaliwa,ndio maana alihisi mkojo unataka kumpenya kwani angeonekana sijui ingekuwaje siku hiyo.
“Yes halloo….Ndio ndio Mr.Bahati Magwira.Ushafika tayari? Mimi nipo njiani kuna foleni kichaa hapa.Nipo Kwa Mlacha,lakini nakaribia kufika..Ahsante”
Mtui alikuwa simuni anazungumza uwongo alifanya hivyo sababu alihitajika eneo hilo haraka sana,baada ya kuweka simu kitandani akarudi tena bafuni, kujimwagia maji.
Hapohapo Marietha akaingia kitandani na kufunua mto,ilikuwa vilevile kama alivyoota kwani bastola ilikuwepo,akaibeba na kuificha ndani ya tumbo lake,sio siri alikuwa akitetemeka kupita kiasi mpaka anaingia chumbani kwake hakuamini kama anayo mkononi na baadaye ingeenda kuuwa watu.Bila kupoteza wakati akavaa nguo zake harakaharaka,akachukuwa mkoba wake na kuiweka bastola yake ndani!
“Eh Mungu naomba unisamehe”
Marietha alisema hivyo huku akitoka nje mkuku mkuku.
“Mama umependesa”
Masai wa getini akamsimfia Marietha lakini hakujibiwa,Marietha alitoka nje ya geti na kukodi pikipiki safari ikaanza hapohapo.
*********
Mtui alihisi kuchanganyikiwa kuliko kawaida,bastola yake hakuiona chini ya mto.Akili yake ilimrudisha nyuma na kuvuta kumbukumbu ni wapi alipoiweka,alikumbuka vizuri sana baada ya kurudi aliiweka chini ya mto lakini hakuiona,alihisi joto la ghafla.
“Au nimeacha kwenye gari?”
Baada ya kujiuliza hivyo alikwapua funguo juu ya meza akatoka nje na kuingia ndani ya gari,akafungua ‘dash board’ lakini hakukuwa na bastola,akaangalia pembeni ya gia lakini wapi.Alihisi kuhaha na aliogopa sana kwani kitu kama hicho kilikuwa hatari mno,kumbukumbu zake zikaanza kumiminika kichwani akaanza kuchora sehemu zote alizopita tangu asubuhi.
“Itakuwa Kwa Malima nini?”
Aliwaza na kuanza kutembea kuingia ndani ili akachukuwe simu yake kisha ampigie rafiki yake ambaye siku hiyo walikuwa pamoja,alivyofika chumbani.Akachukuwa simu na kuanza kumtafuta Bwana Malima hewani,simu iliita na kupokelewa hapohapo.
“Malima”
“Yes Mtui.Leo wapi kwanza tunaenda?Hukuniambia ulivyoniacha”
“Sikiliza Malima,hivi hapo kwako nilivyokuja sikuacha yale mambo?”
“Mambo?Mambo gani?”
“Chuma,Chuma”
“Chuma gani kaka?”
“Bastola”
“Bastola?Hapana sijaona,vipi kwani?”
“Sioni bastola yangu”
“Sema ukweli”
“Nakwambia ukweli,sikutanii”
“Kesi kubwa hiyo,embu cheki vizuri ndani ya gari.Ulivyotoka kwangu ulipitia wapi?”
“Kwa Lilian Hiluka”
“Embu jaribu kumuuliza”
“Aisee,aya sawa”
Mtui alihisi kuvurugwa na tumbo lilianza kumuuma japo hakuelewa la uharo au uwoga,kitendo cha bastola yake kupotea katika mazingira ya kutatanisha kilimuogopesha kwani ingefanyiwa uhalifu yeye ndiye angewajibika vilivyo!Bila kupoteza muda akamtafuta Lilian Hiluka rafiki yake mwingine ambaye wanafanya kazi pamoja na kumuuliza lakini majibu aliyopata yalimchanganya akili yake zaidi,jasho lilizidi kumtitirika na alivyokata simu aliingia kwenye kabati na kuanza kuvuta madraw lakini hakuambulia kitu chochote kile,akainama na kuchungulia chini ya uvungu lakini hali ilikuwa ileile tu.
“Ah aaah atakuwa Mariethaaaa”
Jina la Marietha lilimjia kichwani hapohapo,akakurupuka na kufungua mlango mpaka chumba anacholala Marietha.
“Marietha,Marietha….Ngo ngo ngo”
Akaita huku akigonga mlango kwa fujo,kuna picha ilimjia mbaya ya kutisha na alihisi ni lazima Marietha atakuwa na bastola yake kwani alimshinikiza amfundishe kuitumia.
“Mariethaa Mariethaa”
Hapohapo akanyonga kitasa na kuzama ndani,alivyoingia tu akakumbana na kitanda kitupu.Bila kuuliza chochote akachomoka mpaka getini!
“Masai,Marietha katoka hapa?”
Akauliza huku akihema juujuu!
“Yeye anatoka saa hii saa hii.Mimi nataka suia yeye akadong’a dong’a”
“Kaenda wapi?Hajasema?”
“Siko najua”
Mtui alihisi kubanwa na mkojo,akafungua geti na kutoka nje mbiombio ambapo huko baada ya mita tano kulikuwa na pikipiki nyingi zimepaki.
“Juma,Jumaa”
Jinsi Mtui alivyoita iliogopesha,Juma alikuwa ni kijana muendesha pikipiki hapo mtaani.
“Ebwana kaka wapi?”
“Kuna dada mmoja namuulizia hapa,mlimuona hapa anapita?”
“Demu gani huyo?”
“Mweupe,anaishi pale kwangu”
“Ah huyu anasema Mariethaa”
Dereva mwingine akadakia maongezi,hiyo ilifanya Mtui na Juma wamuangalie.
“Ndio huyo huyo,umemuona wapi?”
“Kaondoka na Dulla”
“Wapi?Una namba za Dulla?”
“Mh,ninazo ndio kwani Marietha yeye hana simu?”
“Hana ndio,mpigie Dulla sasa hivi muulize yuko wapi?”
Jambo hilo lilifanyika dakika hiyohiyo, simu ikatolewa na Dulla akapigiwa ili wamuulize ni wapi Marietha alipo, lakini cha ajabu simu iliita bila kupokelewa,akapiga tena lakini wapi.
“Hapokei simu”
“Embu piga tena”
Simu ikapigwa kwa mara nyingine,kwa bahati nzuri ikapokelewa.
“Dulla uko wapi?Kuna…”
Kabla ya kuendelea mbele zaidi Mtui alikwapua simu sababu aliona anacheleweshwa.
“Dulla,uko wapi?Mimi Mtui”
“Mtui,Inakuwaje kaka?”
“Poa uko wapi?”
“Niko Sinza hapa”
“Sikiliza,upo na Marietha?”
“Ndio nimemshusha sasa hivi”
“Wapi?”
“Kwalalumpa”
“Okay”
Simu ilivyokatwa tu,Mtui akapanda juu ya pikipiki ya bwana Dulla.
“Nikimbize Kwalalumba sasa hivi,haraka sana”
Hapohapo gia ikapigwa na safari ya kwenda Sinza kuanza mara moja,hisia za kuwa Marietha ni lazima anafanya vitu vibaya ilijijenga kichwani mwa Mtui,ndiyo maana alimuhimiza dereva wa bodaboda azidi kuvuta mafuta ili wafike haraka!
***********
Marietha alifikishwa nje ya ukumbi wa Kwalalumpa na dereva wa bodaboda aliyeitwa Dulla saa kumi na mbili kasoro saba,kulikuwa kuna umati wa watu umefurika aliamini kabisa kwa kitendo ambacho angeenda kukifanya kingekua historia kubwa sana lakini hilo hakujali kabisa,ilikuwa ni lazima afanye kile alichokusudia,isingewezekana kabisa kurudisha moyo wake nyuma hata kidogo kwani shetani baya lililoitwa ‘Kibuki’ lilimvaa mwilini.
Moyo wake ulizidi kwenda mbio na kudunda baada ya kusikia vifijo na nderemo kutokea upande wa pili,alivyoangalia vizuri aliuona msafara wa magari unaingia.Muda wake wa kufanya jambo alilokusudia ulifika,hivyo alianza kutembea taratibu kusogea karibu.Niya yake ikiwa kuanza na Issa kisha baadaye amfyatue Katrina na risasi baada ya hapo ajimalize mwenyewe,kwa kufanya hivyo aliamini moyo wake ungetulia.

Alishuhudia gari jeupe aina ya Benz la gharama limefika na lipo katikati, kivyovyote vile ilikuwa ni lazima gari hilo alikuwepo Issa na Katrina,alikuwa ni kama ametabiri sababu mlango ulifunguliwa na alitokeza Katrina akiwa amevaa Shela amependeza Kwelikweli na uzuri wake ulionekana dhahiri mbele yake,hapo ndipo alipoumia zaidi,baada ya sekunde kama tano kupita mlango mwingine ukafunguliwa,mguu uliovaa kiatu cheupe cha gharama ukakanyaga juu ya zulia jekundu,Issa akatokeza akiwa amevaa suti nyeupe pia na suruali nyeusi iliyombana kidogo yaani modo,sio siri alipendeza kuliko kawaida na muda wote alikuwa anatabasamu.Marietha alijisikia uchungu ajabu na alihisi wivu kupita kiasi,hapohapo akaingiza mkono ndani ya mkoba na kuishika bastola vizuri ili aitoe na kumpiga risasi Issa kisha afuate Katrina!



Jinsi Pikipiki ilivyokuwa inakimbia kwa mwendo usiokuwa wa kawaida ilifanya mpaka wapita njia barabarani washike vichwa vyao,kulikuwa kuna kila dalili ya kutokea ajali endapo dereva aliyempakia Mtui asingekuwa makini.Hiyo ilitokana na Mtui kumsumbua dereva kuwa avute mafuta na kukimbiza pikipiki kwani alitakiwa awahi Sinza,ukumbi ulioitwa Kwalalumpa!
“Pita pembeniiiii”
Hiyo ilikuwa ni mara ya nane kwa Mtui kutamka hivyo baada ya kuona mbele kuna vizuizi vya magari,kichwani kwake kulikuwa na vitu chungu mzima vinapita.Alikuwa ana kila sababu na kudhani Marietha huko alipo anafanya jambo la hatari na endapo ingekuwa hivyo basi ni lazima angetupwa gerezani sababu ya uzembe kwani silaha yake ndiyo imetumika kufanya mauaji,hiyo ilifanya azidi kumuhimiza dereva wa pikipiki azidi kuchanja mbuga.
“Tupitie kule Sunsiro,huko tutachelewa”
“Sunsiro kule barabara mbovu”
“Pita hivyohivyo”
“Huku ndio rahisi”
“Nimekwambia pita Sunsiro.Kama hutaki nishushee”
Mtui na dereva wa pikipiki walikuwa wanazungumza kwa sauti za juu ili kushindana na upepo uliokuwa unapuliza,dereva alitii amri ya abiria wake na kufata kile alichoagizwa,ilichukuwa kama dakika kumi na tisa nzima mpaka wanafika Sinza,Lego! Hapo waliingia njia nyingine ya vumbi ili kufupisha ruti.

Dakika tano baadaye wakaibuka Sinza kwa Remmy na kuanza kuutafuta ukumbi wa Kwalalumpa.Hiyo iliwachukuwa dakika nyingine nne mpaka kufika nje ya ukumbi huo ambao ulikuwa una watu wengi sana kwa nje.Mtui alihisi kuchanganyikiwa sababu hakuelewa ni wapi aanze kumtafuta Marietha,alijuwa yupo maeneo ya ukumbi huo lakini hakuelewa ni wapi alipo ndiyo maana alianza kutafuta huku na kule!Kwa mbali aliona Mwanamke amevaa nguo ya rangi nyekundu kwa juu lakini hakuwa mwenye uhakika sababu alizibwa nusu,akaanza kutembea kuelekea upande huo kwani alimfananisha mwanamke huyo na Marietha,akapangua pangua watu lakini alivyofika karibu alisimama sababu hakuwa Marietha,watu walizidi kukusanyika nje ya gari la maharusi na hapo ndipo Mtui alipogeuka upande wa kushoto,akamuona Marietha amesimama anaingiza mkono ndani ya mkoba!Kwa nguvu za ajabu akaanza kuwasukuma watu kama mwendawazimu ingawa walimtukana lakini yeye hakujali.
Marietha alidhamiria kumuuwa Issa na Katrina kisha yeye ajipige risasi ndiyo maana aliingiza mkono ndani ya mkoba ili atoe bastola,alivyoangalia pembeni alimuona Mtui, moyo wake ulipiga kwa nguvu sababu alikuwa anakuja upande wake kwa staili ya kuwapangua watu,hiyo ilifanya atake kufanya tendo lake haraka sana kabla Mtui hajamfikia,kitendo cha kuitoa bastola na kutaka kuiinua Mtui akawa amefika mbele yake na kusimama.
“Unataka kufanya nini wewe mwanamke?”
Mtui akauliza kwa hasira huku akiwa ameshika mkono wa Marietha anamsogeza pembeni ili watu wasione kitendo hicho hatari.
“Nakuuliza unataka kufanya nini?”
Badala ya Marietha kujibu alianza kulia machozi ya kwikwi,mbali na hapo alikuwa akihema juujuu, kifua chake kinapanda juu na kushuka,alivyotaka kumjibu Mtui alishindwa sababu mapafu yake yalijaa hewa midomo yake ikawa inamcheza tu.Hakuna mtu aliyeshuhudia tukio hilo sababu walikuwa gizani.Hapohapo Mtui akachukuwa bastola yake na kuiweka kiunoni,ilionekana alikuwa ameshikwa na hasira ndiyo maana alimuuliza Marietha kwa ukali tena akimuangalia machoni.
”Marietha hivi unajua unachotaka kukifanya,nijibu?Unataka kuleta balaa.Unataka nifungwe?Unataka nifungwe nakuuliza”
Mtui alizidi kufoka na hiyo ilitokana na jinsi mambo yalivyotokea.Isingekuwa juhudi zake za kuwahi wenda yangekuwa mambo mengine ndiyo maana alianza kuvuta picha ingekuwaje kama Marietha angefanya jambo la hatari.Hakuna kitu kingine alichofanya zaidi ya kumvuta Marietha mpaka upande wa pili na kilichomshangaza Mtui ni kitu kimoja tu, baada ya kumuona Katrina yupo ndani ya shela la harusi kuna picha ilianza kujijenga kichwani kwake moja kwa moja kuwa Marietha alitaka kumuua Katrina ili alipe kisasi kwani ndiye aliyefanya mpaka mumewe Deo awepo gerezani ni sawa alikuwa sahihi lakini nyuma ya tukio lililotaka kutokea kulikuwa na historia kubwa ambayo ingemuacha kinywa wazi.
“Marietha nyamaza kwanza,tunarudi nyumbani”
Mtui alilazimika kukodi taxi kutoka Sinza mpaka nyumbani kwake Tegeta,ndani ya gari hakikusikika kitu kingine isipokuwa kilio cha kwikwi kutoka kwa Marietha,bado hata yeye hakuamini kama amepona na isingekuwa Mtui kutokea wenda angekuwa kuzimu ama Jehanam kwani aliamini pepo isingemuhusu sababu kujiua tu ingetosha kupata tiketi ya kuchomwa moto na shetani.
“Nisa..mehee”
“Marietha,tutaongea nyumbani”
Taxi waliyokodi ilizidi kuchanja mbuga na kusonga mbele na ilivyofika saa tatu kasoro walikuwa tayari wamefika Tegeta.
“Subiri nikakupe pesa yako”
Mtui alimwambia dereva taxi baada ya kufika nje ya geti lake.
“Poa broo,lakini huyu sista abaki”
Dereva taxi alidhani anapigwa changa la macho!
“Sawa”
Dakika moja baadaye Mtui alitoka nje ya geti na kumlipa dereva Taxi, Marietha akashuka kisha wote wakaingia ndani,kitendo cha kufika alimuangalia Marietha usoni kwa kama dakika moja nzima.
“Marietha”
Akamuita.
“Abe..e”
“Kwanini ulitaka kufanya mambo ya hatari namna ile?Ulitaka kuozea jela ulitaka namimi nifungwe?Najua ulifanya vile kwa ajili ya Deo,ama kama una mengine niambie”
“Nampenda I..ssa”
“Unampenda naniiiiiiii?”
“De…o”
Marietha alijikuta anachanganya mlenda na Viazi kwa kutaja jina la Issa mbele ya Mtui.
“Miaka kumi na tano ni michache,Deo atatoka Marietha.Jaribu kuvumilia tu na ukumbuke kitu kimoja kuwa kila jaribu lina mlango wake”
“Naelewa,naomba nisamehee”
“Kwanini sasa unachukulia hasira namna hiyo.Marietha usiwe hivyo”
Akili ya Marietha ilivyokaa sawa alihisi kujuta sana kwa kitendo alichotaka kwenda kukifanya,hasira zake zilikuwa zinashuka taratibu na kitu kilichokuwa kimemkaba kohoni kilianza kulainika kadri sekunde zilivyozidi kwenda mbele.
Akapewa maji akanywa na kusisitiza kuwa asamehewe kwa kitendo alichotaka kukifanya kabla,alivyowakumbuka watoto wake wadogo machozi yalimlenga sura ya Deo ilivyomjia kichwani ndiyo alilia kabisa.Jinsi mambo yalivyotokea ilibidi akubaliane na matokeo tu ili maisha yaende kwani kulipiza kisasi kusingebadili jambo lolote lile, hiyo ilimfanya usiku kucha alie machozi akimuomba Mungu wake msamaha kwa jambo alilotaka kulifanya masaa machache yaliyopita nyuma.

************
Siku zilizidi kwenda harakaharaka na hatimaye mwezi ukakatika na siku ya Jumapili ya kila mwisho wa mwezi walitakiwa kwenda kumuona Deo gerezani.Kama wanavyofanya siku zote,walipita kwenye migahawa mbalimbali wakanunua vitu na kupakia ndani ya gari kisha safari ya kwenda gerezani kuanza dakika hiyohiyo.
“Naomba usimwambie Deo kitu kilichotokea”
“Kitu gani?”
“Siku ya harusi ya Katrina”
“Sitakuwa na sababu yoyote ile ya kumwambia”
“Ahsante pia naomba unisamehe”
“Usijali nishasahau,kuwa na Amani”
“Ahsante.Mungu akubariki”
“Amen”
Walikuwa ndani ya gari katikati ya safari na Marietha alimsisitiza sana Mtui asiongee chochote juu ya jambo lililotokea akiamini kuwa Deo ataumia moyo,walivyofika gerezani walimuona Deo na wote walionekana kuchangamka.
“Sasa hivi naanza kuzoea zoea kidogo,nishapata marafiki”
Deo aliwaambia Mtui na Marietha lakini afya yake ilikuwa tofauti na mambo anayozungumza kwani ngozi yake ilibadilika rangi,ikawa kama ina magamba kwa mbali na usoni alipauka.Nywele zake zilikuwa nyingi na chafu zenye vumbi, hakika Maisha ya jela yalimpiga vibaya sana.
“Deo,nakupenda sana mme wangu”
“Hata mimi mke wangu,walete watoto waje kuniona baba yao”
“Haina sababu sitaki wajuwe”
“Nakuomba Marietha fanya hivyo”
“Sawa nitajitahidi”
“Wapo wapi kwani?”
“Lushoto”
“Peke yao?”
“Na Mama zao wadogo”
“Fanya niwaone mwezi unaofuata”
Baada ya maongezi na kuongea mambo mengi mbalimbali walimpa chakula,akala na kufungua maji makubwa ya Kilimanjaro akanywa.Wakati wa kuondoka Marietha alijisikia uchungu moyoni, kumuacha Deo peke yake gerezani, aliamini huko alipo anateseka sana,waliagana, Marietha na Mtui wakaondoka zao!
*******
Kwa Marietha kukaa nyumbani kwa Mtui miezi kadhaa ilifanya afya yake izidi kunawiri,uzuri wake ukarudi, nyama zake zilizopotea zikaanza kuja tena upya,mapaja yake laini na meupe yakawa kama zamani kifupi alitakata, hiyo ilifanya wanaume wenye tamaa waanze kumsumbua wakimtaka kingono.Mbaya zaidi alinunuliwa simu ndogo na Mtui kwa ajili ya mawasiliano ya hapa na pale,hilo lilikuwa tatizo lingine kwani wanaume walimtumia meseji za kumtongoza na wengine walitaka kumuonga vitu vya thamani lakini hakuwa tayari kurudia kosa alilofanya, aliamini huko nyuma aliteleza lakini safari hiyo hakutaka kufanya hivyo na wengi waliokuwa wanamtomngoza Marietha walikuwa marafiki wa Mtui ingawa walijuwa kabisa ni mke wa Deo lakini hawakujali.
“Kwani Deo si yupo Gerezani.Akitoka na biashara yetu inaisha”
Simu hiyo ilitoka kwa Mr.Mohamed Kajeme mfanyabiashara ambaye alikuwa pia ni rafiki mkubwa wa Deo.
“Hapana,nilishakwambia siwezi”
“Kweli utakaa miaka yote hiyo bila kuwa na mwanaume?Umekuwa malaika?”
“Ndio nitaweza”
“Sio kweli”
“Nitaweza”
“Kuwa namimi itakuwa siri yetu.Au upo vipi na Mtui?”
“Kaka mbona maswali mengi,nimekwambia haiwezekani”
Siku hiyo Marietha alichomoa na kukataa akiwa anazungumza na simu,kutongozwa kwake ilikuwa kawaida sana lakini aliendelea kushikilia msimamo wake kwani hakutaka kupanua miguu yake afanye ngono na mwanamme yoyote isipokuwa Deo ambaye yupo gerezani na alidhamiria kumsubiri mpaka miaka kumi na tano ipite ingawa ilikuwa ndiyo kwanza miezi sita imepita tangu Deo afungwe gerezani,hakuwa mwenye uhakika kama angeweza kukaa miaka yote hiyo bila kushiriki tendo la ndoa sababu alikuwa ni mwanamke mwenye hisia na aliyekamilika.

Siku zilizidi kusonga mbele, hatimaye mwezi ukakaribia kufika hiyo ilimlazimu aombe nauli kwa Mtui ili afunge safari mpaka Lushoto akawachukuwe wanaye kwa niya ya kuwapeleka gerezani wakaonane na baba yao na hicho ndicho kilichotokea kwani alienda Lushoto na kumchukuwa Abraham pamoja na mtoto wa kizungu ambaye hapohapo alimpa jina William na hilo lilimjia ghafla akiwa anatembea kuelekea kituo cha basi.
“Wiliam,ngoja basi utanyonya”
“Mamaaa nipee mamaaaa nipee”
Watoto walikuwa wakimsumbua na Abraham alionekana kuwa mwenye furaha ndiyo maana akaita Mama,alikuwa ni mtoto mzuri mno na alishaanza kutembea.Wote akaingia nao ndani ya gari na safari ya kwenda jijini Dar es salaam kuanza.Safari ya kutokea Lushoto mpaka jijini Dar es salaam iliwachukuwa masaa saba hiyo ni kutokana na tairi la basi kupata pancha njiani,ukichanganya na usumbufu wa Abraham na William ilifanya Marietha achoke zaidi na zaidi.Alivyofika Ubungo alipokelewa na Mtui kwa furaha.
“Pole na safari”
“Ahsante shemeji.Abraham msalimie Anco”
“Chikamoo anco”
“Marahaba,huyo mwingine ndiyo…. anyway.Hapa ninamsubiri Mke wangu nayeye anaingia leo wamefika Kimara”
Kuna kitu Mtui alitaka kuropoka lakini aliupiga mdomo wake ‘stop’ hiyo ni baada ya kumuona William mtoto mwenye mchanganyiko wa kizungu yaani ‘Africast’
“Sawa”
Siku hiyo Mtui pia alitakiwa kumpokea mkewe kutokea Mkoani Arusha kwani baada ya kutokea Tanga aliunganisha Arusha huko alikaa zaidi ya miezi mitatu,saa mbili ya usiku ndipo basi la kampuni ya Dar Express liliingia ndani ya lango la Ubungo na hilo ndilo basi ambalo mke wa Mtui alipakia kutokea Arusha.
“Nadhani ndio hao hapo,nisubiri ndani ya gari”
Mtui alisema baada ya kuona basi kubwa limepita kuelekea kwenye maegesho yake maalum,akatembea mpaka kandokando kabisa ya mlango akimsubiri mkewe ashuke.Haikuchukuwa hata dakika moja wakawa wameonana akampokea mkewe mizigo na wote kuingia ndani ya gari.
“Shikamooo”
Ni salamu kutoka kwa Marietha baada ya kumuona Mke wa Mtui amefungua mlango wa mbele na kumkuta yeye ndiye amekaa.
“Marietha,pita nyuma”
Mtui akasema.
“Hapana usijali,wacha nikae nyuma”
“Okay”
Safari ilianza hapohapo ya kurudi nyumbani lakini ilikuwa wazi kabisa Mke wa Mtui hakupendezwa na kitendo hicho cha kukaa kiti cha nyuma, wakati lilikuwa gari la mumewe ingawa hakutaka kulisema jambo hilo waziwazi,kuna picha mbaya ilikuwa inampitia kichwani kuwa ni lazima kuna jambo baya lilikuwa linaendelea kati ya Mumewe na Marietha.
Baada ya kufika nyumbani na kula chakula cha usiku,Mtui alinyeshewa mvua ya maswali baada ya kuingia chumbani.
“Huyu ndio mke mwenza au Awara wako?”
Lilikuwa ni swali lililomlenga Mtui kutoka kwa mkewe.
“Huyu ni mke wa Deo,Marietha au umemsahau?”
“Kwahiyo kama Marietha?Mimi nifanye nini?Deo yupo gerezani kwahiyo ndio mnaamua kumzunguka,unajifanya aluatani?”
“Mke wangu siwezi kufanya hivyo,embu tupumzike alafu nimekumisi kweli,miezi uliyokaa ni mingi nina kiu sana”
“Kiu?Kiu?Hivi unaniona mimi mtoto sana”
“Nitakuelezea kesho sasa hivi nina hamu nawewe mke wangu”
“Nimechoka”
Mtui aliingiwa na kibarua kingine kizito cha kubembeleza unyumba jambo ambalo lilimuwia vigumu kwani mkewe alikataa katukatu kutoa ushirikiano.
“Achana na mimi na huyo kuku na vifaranga vyake kuanzia kesho sitaki kuviona kama unataka amani ndani ya hii nyumba”Mkewe alifoka kwa ukali na kuutupa mkono wa Mtui kando!



Ilikuwa sio rahisi kumlainisha mwanamke huyu mwenye wivu kuliko kitu kingine chochote kile ndiyo maana Mtui ilimuwia vigumu kupata haki yake ya ndoa.Mbali na Mwanamke huyu kugoma kuvua nguo yake ili wafanye tendo la ndoa, alitaka pia Marietha asionekane nyumbani kwake siku inayoitwa kesho,huo ndio ulikuwa msimamo wake.Kwa jinsi matatizo yalivyokuwa yanatokea na Jinsi ambavyo Deo alivyokuwa kwenye matatizo haikuwa rahisi kwa Mtui kumfukuza Marietha hata kidogo.
“Marietha hawezi kuondoka hapa”
Mtui alisema kwa sauti ya ukali kidogo hiyo ilitokana na kusumbuliwa kupata haki yake ya ndoa,akaona nayeye akaze na kama mbwai iwe mbwai.
“Sijakusikia”
“Nasema kuwa Marietha hapa haondoki”
“Embu rudia tena”
“Narudia tena kwa mara nyingine Marietha hapa hawezi kuondoka.Nimeanza kumjua Deo kabla sijakutana na wewe,Deo ni sawa na ndugu yangu.Amenisaidia sana nusu ya hii nyumba kajenga yeye sasa leo hii mkewe yupo kwenye matatizo unataka tumfukuze.Amua unavyoamua lakini msimamo wangu mimi ndio huo.Na ninaomba nikwambie kitu kimoja endapo kitu chochote kikimpata kibaya,nitakuhusisha kwa njia moja ama nyingine,tena ngoja nikakuchukulie RB kesho”
Mtui aliongea mpaka povu likamtoka na alikuwa mwenye jazba kupita kiasi,ndiyo maana alisimama kutoka kitandani na kuanza kutembea huku na kule akiwa amechachamaa na bukta yake fupi.
Huo haukuwa utani kwani katika watu waliokuwa wenye msaada mkubwa katika maisha yake alikuwa ni Deo Karekezi, ndiyo maana hakuweza kumtupa tangu anapata majanga,alikuwa ana kila sababu ya kumtendea wema.
“Ndio hivyo nimekwambia.Marietha atabaki hapa”
Hata siku moja Mtui hakuwahi kufoka kwa sauti namna hiyo,kutokana na sauti kali ilifanya mpaka ipenye na kutoka nje ya Mlango na kumfikia Marietha aliyekuwa anatoka na kuelekea seblen kuchukuwa maji ya kunywa,jina lake kutajwa ilifanya asimame kwanza asikilize malumbano!Moyo ulimuuma sababu alielewa tayari ameingia kwenye matatizo mengine mapya baada ya kuyapiga chenga kwa muda mrefu,kwa maana hiyo ilibidi mwenyewe ajiongeze na asubuhi inayofuata afunge virago vyake na kurudi Lushoto akiamini kwa kubaki hapo atafakaranisha ndoa ya watu jambo ambalo hakutaka litokee hata siku moja kwani aliogopa kuhusishwa na tuhuma hizo mbaya.
Jambo hilo lilimsumbua usiku kucha ndiyo maana hakupata hata lepe la usingizi usiku wa siku hiyo,alitumia muda huo kutafakari maisha yake yalivyokuwa yanaenda kwa ujumla.Tangu alivyozaliwa akakuwa na baadaye akajiingiza kwenye mahusiano ya kimapenzi, kifupi alikusanya matukio mengi tofauti tofauti na nyuma alikuwa ana historia ndefu, mbali na hapo aliamini kwamba ana safari ndefu ambayo hakuelewa mwisho wake ungekuwaje.Alivyomkumbuka Deo gerezani na maisha waliyokuwa wanaishi alijisikia uchungu ajabu na kutamani mambo yarudi nyuma ajikute yupo ndani ya nyumba yao kubwa wanaishi kwa raha mustarehe,bado hakutaka kuamini kuwa mambo yanayotokea ni ukweli sababu kufumba na kufumbua muhimili wa maisha yake uliporomoka kama gorofa lililopigwa na bomu.
“Eh Mungu nimekosea wapi?Kama kweli upo mbona unaacha niteseke namna hii”
Marietha aliwaza baada ya kuwaangalia watoto wake Abraham na William.
Kulivyokucha saa kumi na moja alfajiri aliingia ndani ya kabati na kuanza kuweka nguo zake sawa ndani ya begi lake ili ikifika saa moja kamili aanze safari ya kuondoka zake sababu aliamini ndani ya nyumba hatakiwi kabisa kubaki humo kwani angechochea ugomvi hata hivyo asingeishi kwa raha na watoto wake na ilikuwa wazi kabisa hata sumu angewekewa na mke wa Mtui, jambo hilo lilimtesa kwani kipindi Deo yupo uraiani Mwanamke huyo alimpenda sana na walikuwa marafiki wakubwa.
Alivyomaliza kuweka kila kitu sawa akatoka mpaka seblen,akaketi ili kumsubiri Mtui atoke na kumuaga,akahisi mlango wa Mtui unafunguliwa, akasimama ili amsubiri Mtui lakini moyo wake ukabadili mapigo baada ya kumuona Mke wa Mtui ndiyo katoka!
“Za asubuhi”
Akasamilia.
“Nzuri, Marietha hujambo?Mbona asubuhi asubuhi na mabegi, kulikoni?”
“Nataka kurudi nyumbani”
“Mbona ghafla hivyo?”
“Hapana nimepakumbuka tu”
“Endelea kubaki nasisi Marietha”
Marietha alifananisha sentensi hiyo na unafki kwani usiku wa siku iliyopita alikuwa akipambana na Mtui kuhusu yeye kuondoka kwenye nyumba hiyo,hakutaka kujibu chochote alibaki kimnya na kumtafakari mwanamke huyu mke wa Mtui, alivyokuwa anatabasamu hapo ndipo aliamini msemo unaosema ‘Usione mtu anakuchekea usoni kumbe moyoni ni mnyama’
“Hapana siwezi kubaki kuna mambo ninafatilia hata hivyo nilipigiwa simu tangu juzi nikasema siwezi kuondoka bila kukuona,nilivyosikia unakuja jana nikaona nisubiri ili leo nikuage”
Wakati amebuni uongo ili kumkwepa Mwanamke huyu aliyemfananisha na mnafki,Mtui ndiyo alikuwa anafungua mlango wa chumbani anamaliza kuweka tai yake sawa kohoni,akatokeza seblen.
“Marietha,hujambo?”
“Sijambo shemeji,nataka kuondoka”
“Kwanini?”
“Mimi mwenyewe nashangaa nimemkuta na mabegi hapa seblen.Embu zungumza naye abaki”
Mkewe akadakia japokuwa hakuulizwa yeye.
“Nimemuomba sana abaki nasisi”
Mkewe alizidi kuongea kwa simanzi Mtui alibaki akimuangalia tu bila kumjibu chochote kwani alijuwa kuwa ugomvi ungekuwa palepale endapo Marietha angeendelea kubaki ndani ya nyumba hiyo ingawa waligombana na mkewe kuhusu Marietha lakini hakutaka kuliweka swala hilo wazi.
“Marietha?Kuna nini?”
Mtui akahoji.
“Samahani juzi sikukwambia nilipigiwa simu kutoka Lushoto,wanadai niende kuna tatizo kidogo”
“Mbona ghafla baki hata kesho ili nikusindikize”
“Hapana Shemeji,usijali kabisa kuhusu hilo acha mimi niende”
“Una nauli?”
“Ndio ninayo”
“Sasa zimebaki wiki mbili twende tukamuone Deo,itakuwaje?”
“Usijali nitakuwa nakuja na kuondoka”
“Utaweza kweli?”
“Ndio nitaweza”
Hata ingekuwaje ilikuwa ni lazima Marietha atoke ndani ya nyumba hiyo ili awaachie wanandoa hao nafasi,alisikitika lakini pia alimshukuru sana Mtui kwa wema aliomtendea!Akabeba begi lake dogo na kuanza kutoka nje ambapo huko alifunguliwa geti na Masai,akatoka mpaka nje na kutafuta pikipiki iliyompeleka Mpaka Ubungo terminal.Bahati nzuri alipata basi baada ya kufika na alitabasamu sababu alikumbuka pia mazingira ya nyumbani kwao,aliwakumbuka mama zake wadogo walivyokuwa wanampenda na wanamtunza vizuri.
Alichofurahi na kufanya mawazo yafutike kwake ni kitu kimoja alichokipenda, kukaa siti ya dirishani kazi yake ilikuwa kushangaa miti inayorudi nyuma na kuangalia magari yanavyopita,kimoyomoyo alimuomba sana Mungu wake amfikishe salama salmin.Mungu sio Athuman siku zote kwani alifika Korogwe baada ya masaa matano baadaye,aliteremka na watoto wake pamoja na mizigo mpaka stendi ambapo alitafuta mabasi ya kwenda Soni.
Ilichukuwa dakika arobaini na tano nyingine mpaka basi hilo kujaza abiria ndipo lilipoondoka.Siku zote Marietha akitokea Lushoto milima ya Bumbuli huwa inamkumbusha vitu vingi sana kwani huko ndipo alipokuwa akisoma shule ya msingi,wakazidi kusonga mbele mpaka walipofika kituo kinachoitwa Mkazi,hapo hakukuwa na namna nyingine ya kupanda madaladala yanayokwenda shule ya Maduda ilibidi achukuwe pikipiki.
“Shasha mimi Ngoshiii kule naenda kwa shilingi elfu nane”
Dereva wa bodaboda alimjibu Marietha kwa rafudhi ya kisambaa.
“Ah wapi!Elfu mbili,mimi sijatoka mjini juzi.Mimi ni mwenyeji huku. Hutaki naenda kule juu”
“Shikilisha fanya elfu tano,twende watoto na N’pate pesa ya juishi”
“Sikia kaka nakupa elfu mbili,unaenda au?”
Marietha alikomaa na muendesha pikipiki nayeye akajifanya kukaza,mavazi ya Marietha yalimpagawisha akadhani wenda ni mgeni wa jiji hilo ndiyo maana alitaka kumpiga cha juu!
“Shasha twendee”
Marietha akapanda pikipiki kwa nyuma safari ya kwenda shule ya Maduda ikaanza hapohapo,ilikuwa imetimu saa nane kasoro mbili mchana.
Alivyofika shule ya Maduda akashuka na kumpa dereva ujira wake,akachukuwa barabara ya kwenda kwa miguu,akafika nyumbani kwao.
Jinsi walivyompokea kwa bashasha ilifanya mpaka ajisikie vizuri sana,wakamkaribisha mpaka ndani na bahati nzuri chakula kilikuwa mezani akala akawanyonyesha watoto na kuingia bafuni kujimwagia maji,hakukuwa na kitu kingine alichofanya ni kujitupa kitandani na kulala fofofo kutokana na uchovu wa safari, usingizi ulikuwa mzito kwake!

*********
Maisha ya Marietha yaliendelea kama kawaida na aliridhika kuishi kijijini na ndugu zake,hata Mtui alivyokuja kumchukuwa aligoma bila sababu ya msingi,kilichomfanya akatae ni baada ya kumkumbuka mke wa Mtui.
“Marietha,leo ndiyo siku yenyewe.Unasema huwezi kwenda?Marietha”
“Hapana usijali.Msalimie sana mwambie nitakuja wakati ujao”
“Marietha, kwanini?”
“Sijisikii vizuri,ninasumbuliwa na Maralia”
“Pole sana,kwahiyo nimwambie nini?”
“Msalimie sana”
“Aya”
Mtui hakuwa na sababu nyingine ya kumlazimisha Marietha waongozane mpaka Dar es salaam, alichofanya yeye ni kuingia ndani na kuaga kisha kunywa maji na kuanza safari ya kurudi jijini Dar es salaam bila Marietha ingawa aliumia sana na aliamini pia Deo ingemuumiza kwa njia moja ama nyingine.
******
Siku zilizidi kukimbia kwa kasi kama maporomoko ya maji,hatimaye mwaka ukakatika na ilipita miezi mingi sana bila ya Marietha kwenda jijini Dar es salaam kwenye magereza ya Ukonga kumuona mumewe Deo jambo ambalo lilimuuma sana na sio kwamba hakupenda bali alipata kazi ya upishi kwenye hoteli ya Muhindi iliyokuwa mkoani Tanga,maeneo ya Handeni, mshahara alioupata ulikuwa ni mdogo lakini alijitahidi kuugawa ili watoto wake Abraham na William wale vizuri na nyingine aliweka kama akiba,miezi mitatu mbele alipata pesa ambazo zilizoweza kumfanya apange chumba na kuanza kujitegemea sababu umbali aliokuwepo na hoteli vilimtesa sana,kwake hiyo aliihesabia kama hatua kubwa katika maisha yake.
Akazidi kufanya kazi kwa bidii zote,kilichokuwa kinampa changamoto siku zote ni wanaume waliokuwa wanamtaka kingono.
“Yule binti aliyenihudumia siku ile yuko wapi?”
“Yukoje broo?”
“Mweupe mnene kiasi,ana figa namba nane.Ana macho fulani ya kusinzia”
“Yupi huyo?”
Mwenye sifa hizo katika hoteli hiyo ya Sharif shan Hotel alikuwa ni Marietha peke yake na mteja aliyefika siku hiyo aliifurahia huduma yake mbali na hapo alivutiwa na Marietha.
“Naomba niitie mara moja”
“Sawa”
Marietha alifuatwa jikoni na kupashwa habari,bila hiyana yoyote ile akatembea mpaka kwenye meza ya mzee huyo mfupi mnene kiasi mwenye mvi kichwani.
“Shikamoo”
“Hujambo binti?”
Mzee akapotezea salamu.
“Leo mna chakula gani?”
“Menyu hiyo hapo”
Marietha akatoa kadi ndefu iliyojaa vyakula vilivyokuwepo jikoni.
“Niletee chips kuku na juisi”
“Sawa”
Marietha akageuka na kuanza kutembea hakuelewa huku nyuma anamuumiza mzee wa watu kwa kiasi cha kutosha kwani alikuwa akitingishika kwa nyuma,alivyorudi alikuwa amebeba kila kitu mikononi mwake.
“Hivi hiki chakula unapika wewe?”
Mzee akamdaka Marietha na swali.
“Ndio”
“Kwahiyo unafanya kazi mbili?Kupika na kuhudumia?”
“Ndio”
“Inabidi siku moja uje kunipikia kwangu”
Kufuatia hapo Marietha hakujibu kitu chochote kile aliondoka na kuendelea na shughuli zake za upishi jikoni,siku iliyofuata ilikuwa hivyohivyo kwani mzee huyu alitia maguu na kuagiza chakula tena kwa masharti kwamba Marietha ndiye amuhudumie swala hilo halikuwa gumu kwani Marietha alimchukulia Mzee huyo kama mteja tu.
“Ahsante kwa chakula kitamu”
Mzee akashukuru na kuingiza pesa katikati ya kitabu cha malipo,Marietha alivyoenda mbele na kufungua alikuta maburungutu ya pesa,harakaharaka akarudi mpaka kwenye meza aliyokuwa amekaa mzee.
“Umezidisha pesa”
“Usijali,nime kutip”
“Hapana ahsante”
Alichofanya Marietha ni kurudisha pesa na kuchukuwa jumla anazomdai kisha kuondoka zake.
Mwisho wa siku ilibidi mzee huyo afunguke na kusema ya moyoni lakini ilikuwa tofauti kwani Marietha alimchomolea na kumpiga kibuti na kuanzia siku hiyo hakutaka tena kumuhudumia,sio kwamba alishindwa kumvulia mwanaume nguo yake ya ndani bali aliogopa kurudia kosa la mara ya kwanza, alikuwa yupo tayari kusubiri miaka kumi nne ili Deo atoke ingawa hakuwa mwenye uhakika kama angeweza kustahimili changamoto anazokumbana nazo.
Maisha kwake yaliendelea kama kawaida na aliweza kukaa miezi mingine kumi bila kuguswa na mwanaume yoyote yule kingono, jambo ambalo halikuwa la kawaida kwa mwanamke yoyote mwenye homoni zilizokamilika,hatimaye mwaka wa pili ukakatika akawa hivyohivyo.Furaha yake ilikuwa kwa watoto wake Abraham na Wiliam ambao kila siku walimpa furaha na kazi aliyoipata ilifanya azidi kung’aa zaidi na zaidi.
“Mmmmmh”
Siku hiyo alikuwa chumbani kwake anaangalia sinema iliyoitwa ‘Despirado’ ilivyofika katikati muigizaji aliyeitwa Antonio Banderas alimkunja mrembo kitandani wakawa wanafanya ngono na kupigana madenda kwa fujo,mwili wa Marietha ulisisimka kupita kiasi na damu yake ilimwenda kasi ya ajabu mbali na hapo akili yake ilihama kabisa,akatamni awe kitandani na mwanaume wafanye ngono. Bila kutegemea taratibu akaanza kutoa sidiria yake na kuanza kuyabinya maziwa yake,mkono wake mmoja akaupitisha chini ikulu akaanza kujisugua,hakizufika hata sekunde tano mgodi wake ukawa umejaa ute ute hapo ndipo alipozidi kuzishika chuchu zake huku akitoa miguno puani.
“Aaaaah aaaah shsssss”
Marietha alihema juu juu huku akianza kujenga taswira akiwa kitandani na mwanaume wanafanya ngono!



Ki ukweli alikuwa mbali kihisia na mwili wake ulimsisimka kupita kiasi,hasa alivyoanza kushika chuchu zake na mkono mmoja ukiwa juu ya ikulu yake mwenyewe,kutokana na hali hiyo kuzidi ikafanya mpaka aanze kung’ata midomo yake kimahaba akayafumba macho yake na kuendelea kufanya anachokifanya,kasi ikazidi kuendelea hiyo ikafanya mpaka afike mshindo na kutulia kitandani huku akiwa anahema juujuu,kitendo alichofanya kilimfanya ahisi aibu na hata hivyo alipunguza mafuta kwa kiasi fulani kwani tendo hilo la ndoa hakulifanya siku nyingi sana ndiyo maana alitulia.
Hiyo ilifanya atulie na kuendelea kuangalia sinema hiyo iliyopelekea mpaka akajitomasa mwenyewe!Hapo hakukaa sana akainuka kutoka kitandani na kuingia bafuni ambapo huko alijimwagia maji na kujitupa kitandani,kwa kuwa ilikuwa siku ya Jumapili siku hiyo hakwenda sehemu yoyote ile, kazi yake ilikuwa ni kukaa chumbani na kuangalia sinema moja baada ya nyingine,alivyomaliza hapo aliwapikia wanaye kisha nayeye akala baada ya kuhakikisha wote wamekula.
Akarudi kitandani na kupumzika tena kwani ilikuwa imetimia saa kumi ya jioni na alitumia muda huo kutafakari maisha yake yanavyoenda kiujumla,kitu kilichokuwa kinamsumbua ni hisia za mwili wake ambazo zilikuwa zinampeleka puta kupita kiasi,hakuelewa ni kwa njia gani angekuwa anakata kiu yake kama mwanamke, jambo hilo ndilo alikuwa akilifikiria kila kukicha.
“Nitaweza kweli”
Marietha alijiuliza akiwa yupo kitandani amekaa kihasara hasara,alifanya hivyo sababu alijuwa chumbani yupo peke yake ndiyo maana alikuwa ana uwezo wa kujiachia.
Nyumba aliyopanga ilikuwa kubwa kiasi, yenye vyumba viwili,sable,jiko na bafu la ndani kwa ndani ambapo chumba kimoja walilala watoto wake huku yeye akitumia chumba kingine,maisha kwa Marietha yaliendelea kama kawaida na Abraham pamoja na Wiliam waliendelea kukuwa kadri siku zilivyozidi kwenda mbele zaidi, mbali na hapo walikuwa na afya nzuri kabisa,sio siri watoto wake walikuwa gumzo mtaani na kila mtu alitamani kuwabeba kifupi mwanamke yoyote yule alitamani kuwa na watoto kama Abraham na Wiliam.
“Baba watoto yeye yuko wapi?”
Ni jirani yake mmoja siku moja aliamua kufunguka na kumuuliza swali hilo kwani hakuwahi kumuona Marietha anaingiza mwanaume ndani kwake hata siku moja,jambo hilo lilimpelekea aanze kumdadisi.
“Ni mfanyabiashara hayupo hapa Tanzania”
Alidanganya.
“Hawa wote ni watoto wa baba mmoja?”
“Ndio”
“Una watoto wazuri sana,hongera Marietha.Uwe unatembea tembea jamani sio kila siku kukaa ndani kama utumbo”
“Mimi bado mgeni”
“Mimi si nitakuwepo usijali”
“Sawa nitashukuru”
Mbali na wanawake wenzake kumuonea wivu lakini pia Wanaume walimtamani kingono na walifanya uchunguzi wa hali ya juu kujua ni mwanamme gani ana mahusiano naye,jibu la swali hilo liliwatesa sana na likawa kitendawili ambacho hakuna hata mtu mmoja aliyeweza kukitegua,hakukuwa na mtu hata mmoja aliyejuwa kuwa Mume wa Marietha yupo gerezani kwani hapakuwa na mtu anayemfahamu kinagaubaga!Siku moja akiwa nyumbani kwake jioni alipokea simu kutoka Lushoto kuwa Mtui anamtafuta kwa wudi na uvumba.
“Usimwambie nilipo”
“Yupo sebleni hapa anasema ni dharura sana”
“Anti Ashura,naomba usimwambie ni wapi nilipo.Na namba zangu usimpe tafadhali”
“Sasa nimwambie nini?”
“Mimi sijui lakini kwa sasa hivi sipo tayari kuonana naye,najua anataka niende Dar es salaam.Mimi nitaenda kwa muda wangu isitoshe nipo Kazini huku”
“Sawa usijali,nitajuwa cha kufanya”
“Ahsante”
“Vipi lakini watoto hawajambo?”
“Wote wazima Abaraham kila siku anakuulizia”
“Uwe unamleta mara moja moja,Wiliam?”
“William aliumwa juzi lakini sasa hivi yupo sawa”
“Sawa Marietha,wacha nikutakie jioni njema”
“Nawewe pia”
Marietha katika hesabu zake alitaka aanze maisha mapya ndiyo maana akabadili namba ya simu na alipokuwa anaishi hakutaka mtu yoyote yule ajuwe ndiyo maana hata Mtui alivyotaka kujuwa wapi alipo alimzuia.
Ingawa moyo ulimuuma lakini ilibidi afanye hivyo kwani shabaha yake ilikuwa ni kutafuta kwanza maisha na sio kutegemea watu kwani alijifunza kuwa ‘Maskini hathaminiki’mfano huo ulikuwa hai sababu alipitia matatizo mengi na wengi wao waliishia kumtumia na kumtema kama big g, hiyo ilimfanya awe na usongo wa hali ya juu sana.
Alijitahidi kufanya kazi kwa bidii mno kazini,kuumwa kwake hakukumfanya asitishe kwenda kibaruani.Kadri siku zilivyozidi kwenda mbele ndipo alipozidi kunawiri na kupendeza na uzuri wake ulizidi mara dufu kwani hata pesa ya kununua vipodozi mbalimbali alikuwa nayo, hiyo ikafanya wanaume kila siku wagongane vikumbo wakimtongoza lakini waligonga mwamba kwani Marietha aliwatolea nje na kuwakataa ingawa hawakuonesha kukata tamaa.
“Hizo njia unazotumia kila siku kubuni kunipata, kama nguvu na mbinu hizo ungetumia kutafuta pesa, nina uhakika ungekuwa bilionea”
Ni maneno kutoka kwa Marietha akiwa kwenye moja ya mgahawa siku hiyo, akimwambia kijana anayeitwa Thomas Martin,ilikuwa wazi kuwa kijana huyo alitumia mbinu zaidi ya mia moja lakini zote hazikuzaa matunda kwani Marietha alimkataa na kumpa cha mbavu!
“Marietha..Sikiliza mimi nakupenda mbinu zote nilizotumia ni dhahiri kabisa kuonesha kuwa nakupenda kama ningekuwa na uwezo wa kukupa hii dunia ili nikupate ningefanya hivyo”
“Ha! Haa! Haaa!Usinichekeshe alafu acha utoto wako”
“Usicheke Marietha,nakupenda kweli”
“Tuachane na hizo mada,siwezi kuwa nawewe nilishakwambia tangu muda mrefu sana hukupenda kunisikia,tafadhali achana namimi”
“Marietha siwezi moyo wangu unakupenda sana,nataka nikuoe kama ukinikubalia”
“Thomas,wanawake mbona wapo wengi hapa mjini na ni wazuri tu”
“Sijaona”
“Kwani umenipendea nini?”
“Hilo ni swali dogo lakini jibu lake linahitaji utulivu mkubwa sana”
“Any way sitaki kujua….Acha niwahi kwangu”
“Marietha jaribu kunifikiria”
“Hapana siwezi”
Huo ndio ulikuwa msimamo wa Marietha na alivyosimama nyuma aliacha lawama kwani alikuwa anatingishika yaani hamsini hamsini Mia,akamuacha Thomas Martin anakula kwa macho,bado hakuamini kuwa anaukosa mzigo huo.
******
Siku zote kila shetani ana mbuyu wake kwani Marietha alitokea kumpenda kijana mmoja anayeitwa Michael Muganda ingawa hakumjua kiundani zaidi sababu alimuona mara mbili tu eneo hilo analoishi,siku moja jioni alivyotoka kwenda dukani kununua mafuta ya kula akakutana naye kwa mara nyingine,moyo wake ukawa kama umepigwa na shoti ya umeme.Hapohapo akasahau kilichompeleka dukani.
“Kaka Mambo”
Marietha alijikakamua na kutoa salamu kwa kijana huyu aliyetokea kuunyanyasa mtima wake ghafla namna hiyo.
“Poa”
“Samahani wewe ni mwenyeji wa eneo hili?”
“Hapana”
“Kama nimekufananisha”
Marietha alijaribu kumzoea kijana huyo ambaye alionekana kauzu kidogo, hiyo ilitokana na kumjibu mkato kwani ilionekana hakutaka mazoea kabisa, jambo hilo ilimfanya Marietha azidi kuumia zaidi.
“Nipe na Soda take away mbili”
“Poa”
Michael Muganga alizungumza na muuza duka na jinsi alivyokuwa akiongea kwa sauti ya kistaarabu ilifanya mpaka Marietha asisimke mwili.Hata alivyoondoka alibakia akimwangalia mpaka anaishia kona ya mwisho na kukata.
“Samahani kaka, huyu Michael anaishi wapi?”
“Mtaa wa nyuma hapo”
“Na nani?”
“Kwa kweli sijui ila sio mwenyeji wa huku,amekuja tu likizo nadhani anasoma chuo”
“Oh okay sawa,akija mwambie nimemsalimia”
“Poa”
“Nipimie mafuta lita moja na nusu”
Tangu siku hiyo Marietha hakutulia, kutwa kiguu na njia dukani ili tu aonane na Michael lakini zilipita siku tatu hakuweza kumtia machoni hiyo ilimkosesha raha.
“Na leo pia hukumwona?”
Siku hiyo Marietha alimuuliza muuza duka kwa mara nyingine.
“Hajafika hapa”
“Atakuwa wapi?Kwao unapajua?”
“Ndio”
“Nielekeze”
“Mtaa wa nyuma hapo,ukipita nyumba ya kwanza utaona nguzo.Baada ya nguzo nyumba ya kwanza ya pili.Nje ina michongoma ndio hapo”
“Aya kaka Ahsante”
Siku hiyo Marietha alijitosa kimasomaso na alikuwa tayari kuusikiliza moyo wake unataka nini,hakuwa tayari kuumia kirahisi hata kidogo!Akaanza safari ya kutembea alipoelekezwa ingawa kulikuwa na giza totoro lakini alipiga moyo konde,alivyofika moja ya kona akakunja na kuupita mstimu akazidi kusonga mbele zaidi.
“Nyumba ya michongoma ndiyo hii”
Marietha alijaribu kuvuta maneno ya muuza duka aliyemuelekeza,akafika mpaka nje ya nyumba na kusikia kelele ya mziki.
Moyo wake ukaanza kwenda mbio na alihisi uwoga umemwingia,akatamani kuondoka lakini maji alikuwa teyari keshayavulia nguo.
“Ngo! Ngoo! Ngooo!”
Akajitosa na kugonga mlango,akarudi nyuma kidogo kwani alikuwa bado ana kauoga fulani.Akahisi vishindo vya mtu vinakuja baadaye mlango ukafunguliwa,moyo wa Marietha uliishiwa nguvu kwani alitoka mwanamke akiwa amevaa taulo moja na alitanda mlangoni.
“Karibu,unamuhitaji nani?”
Binti huyo mdogo aliuliza huku akimtizama Marietha kuanza juu mpaka chini yaani kwa staili ya kumpandisha juu chini chini juu.
“Nadhani nimepotea samahani”
“Ulikuwa unaenda wapi?”
“Usijali”
Baada ya kujibu sentensi hiyo ya binti huyu mdogo akatokeza Michael Muganda na kumtizama Marietha, machoni.Lakini kabla ya kuongea chochote alimshuhudia Marietha anaondoka zake bila kugeuka nyuma kwani alibanwa na wivu ajabu na alichukulia moja kwa moja kuwa hawezi tena kumpata Michael,hiyo ilimfanya afike kwake, apitilize chumbani na kujitupa kitandani akiwa mwenye mawazo chungu mzima kichwani,sura ya Michael ilikuwa ikipita kichwani kwake mara kadhaa tena wakati mwingine alidiriki hata kumvuta kihisia na kuyapapasa maziwa yake huku akijitomasa mwili mzima!
“Kwanini nimempenda huyu mkaka ghafla namna hiii”
Marietha alijishangaa mwenyewe wakati mwingine alilihusisha jambo hilo na ndumba!
“Au kaniendea kwa waganga,maana sio kwa staili hii ya kumpenda”
Huyu alikuwa Marietha akitafakari usiku na mchana,siku mbili nyingine zilipita akiwa anamuwaza Michael pamoja na mwanamke aliyemkuta naye.
“Hata kushea tutashea tu,potelea mbali”
Yote hayo yalipita kichwani mwa Marietha na alivyorudi kutoka kazini siku hiyo alinyoosha mpaka dukani hapo aliacha namba zake za simu.
“Akifika siku yoyote mwambie anipigie ni muhimu sana.Jina langu nimeliandika hapo juu ya karatasi”
“Sawa dada,nitamwambia”
“Nipimie na mchele kilo tatu”
“Sawa”
Alijilazimisha tu kununua Mchele lakini shabaha yake tangu alipotoka ilikuwa ni kuacha namba zake za simu ili apewe mwanaume anayeunyanyasa moyo wake siku zote.
Kufuatia hapo muda wote alikuwa ana simu yake ya mkononi, kuanzia siku hiyo na kila ilipoita hata akiwa bafuni basi atatoka na mapovu ili akaangalie kama hakuwa Michael.
Siku hiyo alivyotoka kupika simu yake iliita,alikimbia mpaka pembeni na kujifuta mikono, moyo ulikita kwa nguvu sababu aliamini ni lazima angekuwa Michael anapiga kwani namba zilikuwa ngeni,haraka akaikwapua na kuiweka sikioni.
“Marietha mimi ni Golden Tende.Mbona hupokei simu yangu? Nimeamua kukupigia na namba tofauti.Mbona unanifanyia hivyo si…”
“Tende,nilishakwambia ukome na achana namimi hivi Kiswahili hukielewi vizuri?Ukome kama ulivyokoma kunyonya kwenye ziwa la Mama yako sawaaa,umenielewa?”
Kitendo cha kupokea simu hiyo kiliibua hasira kutoka kifuani mwa Marietha na kuanzia hapo Bwana Golden Tende aliogeshwa mvua za matusi na kuchambwa kuanzia juu mpaka chini,hapohapo akakata simu na alivyoiweka chini ikaita tena!Ilikuwa namba nyingine ngeni,akaitizama kwa muda!Akaipokea na kuiweka sikioni.
“Halloooo”
Marietha alisema lakini upande wa pili,ulikuwa kimnya na kwa mbali alisikia sauti zinabishana.Moja ya kike na moja ya kiume.
“Babra acha utoto,embu hiyo simu.Sasa hivi utanikera”
Upande wa pili wa simu ulisikika bado Marietha aliendelea kusikiliza.
“Wewe Marietha.Mimi naitwa Babra Ramadhan!Naomba uachane na Michael,sawa wewe kahaba.Umenielewaaa?”
Ilikuwa ni sauti kali ya kike kutokea upande wa pili ikimtukana,hiyo ilimfanya azidi kuumia moyo zaidi.


Marietha aliendelea kuogeshwa mvua ya matusi na hazikuisha kwani mwanamke huyo aliendelea kumpolomoshea matusi ya nguoni,hiyo ilifanya ashindwe kuvumilia na kukata simu.Hakukaa sawa simu yake ikaanza kuita na namba ilikuwa ileile,hakupokea lakini ikaita tena!Alielewa vizuri sana nini maana ya kupokea simu hiyo, ndiyo maana akaacha mpaka simu ikate yenyewe.
“Titiiiiii”
Ni ujumbe wa meseji uliosikika kutokea kwenye simu,taratibu akaichukuwa ili kusoma ujumbe huo alioamini kuwa kabisa ulitoka kwa mwanamke aliyejitambulisha anaitwa Babra,ni kweli ilikuwa ni kama ametabiri.
‘UKAE MBALI NA MICHAEL KAMA UNATAKA AMANI KATIKA HII DUNIA TENA UKOME MALAYA MKUBWA WEWE’
Huo ndio ujumbe uliotoka kwa mwanamke huyo aliyeonekana kuwa na hasira sana tena mshari,hiyo ilimuumiza sana Marietha moyo.
Hakuelewa ni kwanini mtima wake umetokea kuanguka kwa kijana huyo Michael, tena kwa kipindi kifupi namna hiyo,katika siku ambayo aliumia ni siku hiyo baada ya kutoka kutukanwa matusi!Hiyo ilipelekea mpaka akose lepe la usingizi usiku,muda wote alitumia kumfikiria Michael ingawa alitukanwa.
“Au niachane naye tu.Lakini ninampenda,sijui nifanye nini?Eh moyo sukuma damu si vingine,mbona nateseka hivi”
Marietha alitafakari usiku wa manane akiwa kitandani amelala chali macho yake yanaangalia juu,ilikuwa ngumu kwake kuamini kuwa atamkosa Michael kizembe namna hiyo.
“Wanaume wengi wananipenda iweje yeye ashindwe kunipenda?Nitafanya kitu chochote kile”
Marietha alijijuwa fika kwamba yeye ni mzuri, tena mrembo wa kuvutia na kwa mwanaume kama Michael kumpata ilikuwa ni sawa na kuweka tonge la ugali mdomoni,hilo aliliamini asilimia zote mia moja kama angeamua kumfungia kazi.
Kulivyokucha asubuhi ya siku iliyofuata, aliamka na kujiandaa ili aende kazini huku nyuma akiwaacha watoto wake kwa jirani kama anavyofanya kila siku akienda kibaruani.Ratiba yake siku zote ilijulikana ya upishi na kuhudumia wateja,muda wa chakula cha mchana ilikuwa ni lazima zamu yake ishikwe ili yeye akale na kupumzika kwa dakika nyingine ishirini lakini siku hiyo hakufanya hivyo badala yake alimtafuta kijana mmoja wa jikoni aliyefahamika kwa jina la Kibakuli.
“Marietha vipi tena?”
Kibakuli mpishi wa jikoni aliuliza kwa mshangao kwani yeye na Marietha hawakuwa na mazoea kwa sana, ndiyo maana alijiuliza mara mbilimbili akionekana mwenye mashaka,wakati mwingine aliona labda zali la mentali limemdondokea kwani katika wanaume waliokuwa wanamtamani Marietha yeye alikuwa mmoja wapo lakini hata siku moja hakuthubutu kufungua kinywa chake kusema ya moyoni,kifupi alikuwa domo zege!
“Kuna kitu naomba unisaidie”
Marietha alianza mazungumzo wakiwa mezani siku hiyo kwenye kona ya mwisho.
“Nipo tayari.Kitu gani?”
“Nitakupa namba uipige alafu umuulizie mtu mmoja anaitwa Michael”
“Enhee….”
“Ukisikia sauti ya kike muulizie Michael,umenielewa Kibakuli?”
“Sawa nimekuelewa”
“Ukisikia sauti ya kiume pia hivyohivyo”
“Hakuna shida”
“Subiri nikupe namba”
Marietha akatoa simu yake na kutafuta namba zilizompigia usiku wa jana yaani ‘received calls’ akaichukuwa namba na kuanza kumtajia Kibakuli.
“Weka loudspika”
“Poa”
Kibakuli akafanya kama alivyoagizwa,akaweka namba kisha kubonyeza loudspika ili simu ikipokelewa Marietha nayeye aweze kusikia,baada ya kuruhusu simu itoke ndani ya sekunde moja ikaanza kuita.
“Halloo”
Moyo wa Marietha ukapiga kwa nguvu aliyepokea alikuwa ni mwanaume na moja kwa moja ilikuwa ni lazima angekuwa Michael, mwanaume anaeunyanyasa moyo wake.
“Naomba kuzungumza na Michael”
Kibakuli akafanya kama alivyoambiwa.
“Wewe nani?”
“Mimi naitwa Kibakuli,namuuliza Michael”
“Kibakuli wa wapi?”
“Michael mimi Marietha”
Marietha alishindwa kujizuia hapohapo akaingilia maongezi kwani hakuweza kusubiri tena,jinsi mapigo yake ya moyo yalivyokuwa yanaenda mbio ikafanya awe mwenye hamu kubwa sana,ndiyo maana hakuwa mwenye subira.
“Michael”
Marietha akaita tena sababu upande wa pili ulikuwa kimnya.
“Yes,nani mwenzangu?”
“Mariethaa”
“Mariethaaa,Mariethaaa,Mariethaa yupi tena?”
Kufuatia swali hilo ilimfanya Marietha achukuwe simu na kusimama na kutoka pembeni kwani hakutaka Kibakuli ajuwe nini anataka kuongea,akatoka mpaka nje kabisa na kuanza kujieleza kinagaubaga!
“Pole na mambo yaliyotokea jana,yule demu ni mkorofi sana.Nambie za masiku?Upo wapi?”
“Nipo kazini,naweza nikakuona leo?”
“Mimi nipo,wapi tuonane?”
“Njoo kwangu, au?”
“Kwako?Unaishi wapi?”
“Kwenye nyumba ya mzee Iddi”
“Sawa nitakuja ingawa sio mwenyeji sana hiyo mitaa,saa ngapi?”
“Nikitoka kazini nitakwambia”
“Poa poa”
Ilikuwa ni kama barafu la baridi limepita ndani ya moyo wake kwa namna ambavyo alikuwa mwenye furaha baada ya kuongea na Michael kipenzi cha roho yake,hakuamini kama mambo yangekuwa marahisi namna hiyo kwani alivyomuona mara ya kwanza na kumsalimia ilikuwa ni tofauti na walivyoongea, hiyo ilimpa nguvu nyingine mpya na kutamani asogeze muda mbele atoke kazini ili aonane na Michael.
Alivyorudi jikoni,aliendelea kufanya kazi kama kawaida lakini akili yake haikuwa hapo hata kidogo,alikuwa akifikiria mikakati mbalimbali ya jinsi atakavyokuwa na Michael baadaye na njia gani atumie siku hiyo kumnasa,sio siri siku hiyo alitafakari kupita kiasi.
Hiyo ilipelekea mpaka atake kuunguza chakula.Kwa Marietha ratiba yake ilikuwa tofauti kabisa na siku nyingine akiwa anatoka kazini badala ya kukaa kidogo na kupiga stori za hapa na pale yeye alinyoosha moja kwa moja mpaka nyumbani kwake ambapo alipita kuwaangalia wanaye.
“Wamelala”
“Basi usiwaamshe nitakuja baadaye kuwachukuwa”
“Sawa”
Hakutaka kuwachukuwa wanaye siku hiyo sababu alikuwa ana ugeni mzito nyumbani kwake,kitendo cha kufika na kufungua mlango alianza kufanya usafi wa hali ya juu.Akaingia chumbani akaweka kitanda vizuri,akachukuwa ‘airfresh’na kupuliza chumba kizima.Alivyohakikisha kila kitu amekiweka sawa akaingia bafuni kujimwagia maji kisha kuvaa sketi fupi na laini iliyofanya umbo lake namba nane lijichore vizuri,hapohapo akachukuwa simu na kumtafuta Michael hewani.
“Nishatoka kazini”
Marietha alisema baada ya salamu za hapa na pale.
“Ulisema kwa Mzee Iddi?”
“Hapo hapo,chumba cha kwenye kona kabisa.Kina grili la kijani”
“Sawa nakuja,nipe dakika tano”
Sentensi hiyo ‘Nipe dakika tano’ilimfanya Marietha aone kama ameambiwa subiri mpaka mwakani kwani kwake dakika zilikuwa nyingi kwa namna ambavyo alivyompania Michael,hiyo ilifanya mpaka ashindwe kutulia kitini,mara atembee mara ashike rimoti ilimradi vurugu tupu.Hiyo ilitokana na kiraruraru alichokuwa nacho, ikapelekea mpaka aanze kujenga taswira ya jinsi atakavyofanya endapo Michael akiingia.
“Ngo ngo ngooo”
Mlango wake ukagongwa,mapigo yake ya moyo yakazidi kwenda kwa nguvu,akatembea mpaka dirishani na kuvuta pazia, akumuona Michael amesimama mlangoni.Ingawa ilikuwa jioni ya saa kumi na moja lakini alifunga pazia sababu hakutaka watu wanaopita nje wamuone ndiyo maana alilifunga.Akapita mbele ya kioo haraka na kujikagua kwa mara ya mwisho,akapandisha maziwa yake juu kiasi na kuanza kutembea kuelekea mlangoni,akafungua.
“Karibu”
Akasema huku akiachia tabasamu mwanana.
“Ahsante”
“Karibu ndani,usiogope”
Michael alisita kidogo kwani mavazi aliyovaa Marietha yalikuwa ni hatari sana, hiyo ilimfanya mpaka yeye asisimke mwili.
“Upo mwenyewe?”
“Ndio”
“Shemeji yuko wapi?”
“Michael,karibu bwana acha maswali kama tupo bungeni”
Nyumba aliyopanga ilikuwa na seble ndogo ya kiaina,hivyo alimkaribisha Michael kwenye moja na viti vilivyokuwa pembeni.
“Unakunywa nini?”
“Nipe maji tu”
Marietha aliingia chumbani kwake lilipokuwa friji na baadaye akafika na jagi la maji ya kunywa pamoja na glasi akamimina na kuweka juu ya stuli,kichwani alitafakari njia gani amuanze nayo Michael kwani aliishiwa pozi na kupata kigugumizi cha ghafla.
Kwa mara ya kwanza siku hiyo ilikuwa kumtamani mwanaume na alitamani afanye naye ngono siku hiyohiyo,ndiyo maana aliweweseka.Hakuelewa ni wapi aanzie kwani katika maisha yake hakuwahi kumtongoza mwanaume!
“Michael nakuja mara moja”
Marietha aliaga na kuingia chumbani huku nyuma akimuacha Michael peke yake seblen.
“Hapa inabidi ninunue kiroba tu,nikate mshipa wa aibu.Sina jinsi nina hamu sana siwezi kumuacha aondoke hivi hivi,nitajilaumu sana.Hata punda akifa ilimradi mzigo ufike”
Hivyo ndivyo alivyoamua, ilikuwa ni lazima siku hiyo afanye ngono na Michael kwa njia moja ama nyingine hata ikiwezekana ambake,kutokana na miyemko yake kupanda sana licha ya yote hakuwahi kufanya tendo hilo kwa muda mrefu sana!Bila kuwaza kitu kingine chochote akachukuwa mkoba wake na kutoa pesa ambapo alivuta kanga na kujifunga,akafungua mlango.
“Michael nakuja sasa hivi nisubiri”
“Uwahi basi,maana nataka kuondoka”
“Usijali,sasa hivi usiondoke lakini kabla sijarudi”
Marietha alitoka nje,akatembea harakaharaka mpaka dukani ambapo alinunua kiroba cha Zanzi rangi yake ilikuwa kama ya maziwa na ilikuwa tamu kidogo kwani muuza duka ndiye aliyemwambia.
“Niongeze vingine viwili,hii ni tamutamu?”
“Hiyo kama maziwa,sio chungu”
“Mh!Poa poa”
Jumla akawa amenunua viroba pakiti tano,hakuwahi kufanya hivyo kabla, hiyo ndiyo ilikuwa mara yake ya kwanza.Hakutaka kupoteza wakati alivyopiga hatua tatu,akachomoa kimoja na kukichana na meno,akakifyonza,akachukuwa cha pili akafanya hivyohivyo pia.Cha tatu pia alkadhalika,kisha akaanza kutembea kuelekea getini,akaingia mpaka ndani ambapo baada ya kufika alianza kuhisi kama kizunguzungu kwa mbali hivi.
“Enhee Michael,ndiyo nini kunipa demu wako anitukane siku ile?Huna hata hayaaa”
Marietha akaanza kuropoka hakuwa yeye bali ni nguvu ya pombe kupanda kichwani.
“Sijampa simu.Alichukuwa karatasi ndani ya suruali yangu,ile karatasi uliyoandika namba za simu”
“Muongo nyamaaazaaaa,unanidanganyaaa.Ujuee niliumiaaa sanaaa”
Marietha alianza kuongea akitolea sauti za puani na hapo tayari mshipa wake wa aibu ulikatika hivyo alikuwa anaropoka,hakuogopa tena kwani alitembea mpaka Kwa Michael na kumsogelea karibu,akamvuta mdomoni na kutoa ulimi.
Ilikuwa ni kama Michael nayeye anasubiri kitendo hiko kitokee sababu aliudaka ulimi vizuri mdomoni wakaanza kunyonyana midomo yao kwa fujo,kati ya watu hawa wawili mmoja wapo alikuwa ana moto zaidi na huyo sio mwingine bali ni Marietha kwani hapo hapo alianza kutoa nguo zake,akatupa kanga pembeni na kuvua kimini alichovaa.Wakati Marietha anafanya hayo yeye Michael alikuwa ana kazi ya kuvua mkanda wake harakaharaka,akatoa shati la juu na kutupa jeans kando kabisa.Akamvuta Marietha juu ya Kochi na kumkunja vizuri ambapo hapo walianza kunyonyana midomo!Marietha alipagawa zaidi baada ya shingo yake kuanza kunyonywa huku mkono mmoja wa Michael ukiwa kwenye mgodi wake,alihisi roho yake inaacha mwili kutokana na raha alizokuwa anahisi ndiyo maana alianza kukinyonga kiuno chake taratibu,kutokana na midadi kumpanda zaidi akachukuwa mkono wake na kushika ndizi ya Michael ambayo tayari ilikuwa imetuna na misuli ipo nganganga,mwenyewe akachukuwa ndizi na kuitumbukiza ndani ya mgodi wake akaanza kukinyonga kiuno.
“Aaaaah aaaasshh aaaaah”
Hiyo ndiyo miguno aliyokuwa anatoa Marietha akiwa juu ya kiuno cha Michael,mtanange ulizidi kuendelea na Marietha alipinduliwa akalazwa chali,Michael akachukuwa mguu wake mmoja akauweka begani.Sio siri siku hiyo Marietha alikunjwa na walivyomaliza Seblen waliingia chumbani ambapo huko,mchezo huo uliendelea kama kawaida.
“Ah ah ah Mic..hael Ah ah aaah ah ah”
Marietha alizidiwa na kelele alizotowa zilikuwa ni nyingi hiyo ilifanya mpaka Michael amuwekee kiganja cha mkono mdomoni mwake ili kumzuia lakini haikusaidia kwani hata majirani waliokuwa wanapita nje walisikia kelele za Marietha akiwa katika utamu,mechi iliisha baada ya dakika kumi na sita baadaye na Michael alisimama na kutembea mpaka seblen.
“Kumbe simu yangu iliiita”
Ni Michael ndiye aliyesema baada ya kuangalia simu yake,hakukaa sana simu yake ikaanza kuita tena na alivyoangalia aliona jina ‘ANCO MTUI’akatafakari kidogo na kuweka simu sikioni.
“Shikamoo Anco”


“Marahaba hujambo Michael”
“Sijambo,vipi huko?”
“Huku salama”
“Chuo hukuniambia mnafungua lini”
“Ni baada ya mwezi mmoja Anco”
“Utanitumia mahitaji yako kesho.Nitumie na ile karatasi ya ada ya semester”
“Sawa anco”
Mtui alimaliza kuongea na simu usiku wa saa mbili,pembeni alikuwa na mke wake.Katika jukumu zima la kumsomesha Michael Muganda,alilivaa yeye kwani alikuwa ni mdogo wake na mkewe yaani yeye na Michael walikuwa mtu na shemeji yake.Walimpenda sana Michael sababu alikuwa ana juhudi darasani,tangu anaanza kidato cha kwanza yeye ndiye aliyemsomesha na mpaka anafika chuo kikuu pia.
Hio ilikuwa furaha kubwa sana kwao kwani alikuwa anaenda kuhitimu masomo yake ya ngazi za juu.Kuna kitu kilichokuwa kina mtesa Mtui siku zote katika akili yake,kifungo cha Deo gerezani,hilo lilikuwa ni pigo kubwa sana na kilichomuumiza zaidi na zaidi ni kuhusu Marietha kukataa kufika gerezani, hakuelewa nini sababu iliyofanya mpaka Marietha abadilike namna hiyo kwani hata alivyoenda Mkoani Tanga wilayani Lushoto kumsaka, hakuambulia kitu na hakuna hata ndugu mmoja aliyekuwa tayari kusema ni wapi Marietha alipo.
“Wiki ijayo naenda kumuona Deo”
Mtui alimsemesha mkewe siku hiyo baada ya kutafakari kwa muda mrefu kidogo.
“Anaendeleaje huko?”
“Hivyo hivyo tu.Analalamika sana,anahitaji kumuona mkewe na watoto”
“Kwani wewe si ulienda kwa Marietha?”
“Nilienda,si nilikwambia ilivyokuwa”
“Kwamba?”
“Sikumuona na hakuna hata mmoja wao aliyeniambia ni wapi Marietha alipo.Simu yake haipo hewani”
“Sasa Deo alivyokuuliza ulimwambia nini?”
“Sikupata jibu strait la kumpa,nilipata kigugumizi”
“Ungemwambia ukweli”
“Hapana,atajisikia vibaya.Wakati mwingine inabidi uufiche ukweli ili umpe mtu moyo”
“Aya utamwambia nini sasa ukienda tena?”
“Nitajua hukohuko nikifika, Deo ni zaidi ya rafiki yangu ujuwe,ni muelewa yule ni msomi na mtu mzima.Nitajua cha kumwambia”
“Aya,mimi nipo bega kwa bega nawewe!Lakini Marietha ananishangaza sana,mumewe yupo kwenye matatizo alafu yeye anakaa mbali”
“Bwana wee,tuachane na hayo.Nina kiu ya juisi iko wapi?”
“Nawewe utamaliza hiyo juisi sasa,kila wakati”
Hayo ndiyo yalikuwa majadiliano kati ya Mtui na mkewe, usiku huo wakimzungumzia Deo na familia yake kwa ujumla,hakuna hata mmoja kati yao aliyekuwa tayari kukubali matendo aliyokuwa anafanya Marietha ya kukata mguu kwenda kumuona Mumewe gerezani.

Siku zilijisogeza harakaharaka na hatimaye mwezi mwingine ulikatika,iliyokuwa inasubiriwa ni siku inayoitwa Jumapili ili Mtui aende gerezani kumuona rafiki yake kipenzi.Baada ya kutoka kanisani na mkewe,waliunganisha mpaka soko la Tegeta nyuki, huko walinunua vyakula mbalimbali kama nyanya,karoti,vitunguu,mchele,viazi na viungo vingine vya chakula.
“Leo nitampikia Deo”
“Si nitachelewa sasa”
“Hapana,pilau dada keshaanza kupika.Naenda kurost viazi basi.Kila siku kununua chakula nje nadhani hata yeye amekichoka”
“Hilo nalo la msingi”
Kila kitu cha kupika chakula kilinunuliwa na mpaka nusu saa linakatika walifanikiwa kujaza mifuko miwili ya vitu vya kupika,wakaingiza mizigo ndani ya gari na safari ya kurudi nyumbani kwao kuanza mara moja.Kitendo cha kufika tu mke wa Mtui aliingia jikoni na kuanza kumenya na kuchonga viazi.
“Washa hilo jiko bandika haya maji,pilau tayari limeiva?”
“Hapana Mama”
“Hivyo vitu vingine weka kwenye friji,nadhani vitatosha mpaka mwezi huu unaisha”
“Ndio vitatosha Mama”
Mke wa Mtui alikuwa ametanda jikoni siku hiyo anakalangiza,yote hiyo alifanya kwa ajili ya Deo na alihakikisha anapika chakula kizuri,ni kweli mwanamke huyu akiingia jikoni huwa hakosei hata kidogo kwani baada ya dakika themanini kile alichokuwa anataka kupika kilikuwa teyari, akavuta ‘Hotpot’ na kuweka mboga vizuri,pilau lilivyoiva akaepua na kuliweka ndani ya hotpot.
Akachukuwa Kuku wa kukaanga kwenye friji na kuwabanika kwenye oveni,walivyokuwa tayari akawafunga vizuri.Mpaka inafika saa nane kasoro msosi ulikuwa tayari umeiva.
“Sasa utakula kwanza au?”
“Hapana,changu nifungie nitakula na Deo kulekule”
“Sawa,msalimie sana.Mwambie nitakuja siku moja kumuona”
“Hakuna neno,naacha simu moja.Nitafute kwenye Airtel ndiyo nitakuwa hewani”
“Okay Darling”
Mtui akaingia ndani ya gari akiwa na vyakula mikononi,alivyoweka vizuri akalitia moto na safari ya kwenda gerezani kuanza mara moja!Haikuwa kazi ngumu, kama siku zote kwani alivyofika askari magereza alimtaka aonje chakula kwanza,baada ya kufanya hivyo waliingia moja kwa moja na kumsaka Deo, dakika moja baadaye akatokeza, wote wakatabasamu.
“Mtui,nilidhani leo hutokuja”
Deo akaongea huku akitabasamu kidogo, kuashiria kuwa mambo ni shwari.
“Chakula shemeji yako kapika leo kilichelewa kidogo kuiva.Ndiyo maana,leo kapika mwenyewe”
“Fungua basi,maana nina njaa balaa,leo sikula chakula hapa.Nikawa nasubiri”
“Basi leo utapenda,namimi leo sijala”
Mtui akaweka mfuko mezani na kutoa hotpot,sahani mbili kisha kuzitenga.Akaanza kupakua taratibu na baadaye akaweka mboga.Baada ya hapo Deo alifuata,akapakua chakula na kuanza kujichana chakula ambacho kwake kilikuwa kitamu kuliko kawaida.
“Marietha anaendeleaje?”
“Bado anaumwa umwa Malaria lakini hali yake sio mbaya sana”
“Jitahidi uje naye mmmmh mmmmh usisahau”
Deo aliongea akiwa anatafuna mnofu wa nyama ya kuku,baada ya hapo Mtui alitoa chupa kubwa ya soda ya Fanta,akamimina kwenye glasi wote wakaanza kushushia! Maisha hayo yalimkumbusha mbali sana Deo na alikuwa ana kila sababu ya kumshukuru Mtui kwa kila kitu anachokifanya kwani aliamini huyo ndiye ndugu yake aliyebaki naye.
Ndugu zake wa damu walikuwa hai lakini aligombana nao kipindi cha nyuma ndiyo maana mpaka anapata matatizo hayo hakuna hata mmoja aliyefika kumuona na marafiki zake aliokuwa anakunywa nao na kutanua wote walimtema, baada ya kukumbwa na matatizo licha ya yote alikumbuka sana kipindi alivyo mtusi Mama yake mzazi,matatizo hayo kutokea aliyajumuisha kama laana kutoka kwa Mama yake.Walivyomaliza kula wakaendelea kuzungumza mambo mengi sana hususani maisha yanavyoenda kwa ujumla.
“Nishazoea tayari,mara ya kwanza iliniwia vigumu sana”
“Utatoka Deo,siku zinakimbia sana.Ipo siku tutakaa tena baa utaniambia Mtui kweli uliniambia siku hazigandi”
Mtui alimpa moyo rafiki yake, akiwa anampiga piga begani,muda ulizidi kwenda na hatimaye wafungwa wote wakarudishwa ndani, hapo ndipo Deo alilengwa na machozi.
Ilikuwa wazi kabisa kwa mara ya kwanza Deo kuishi gerezani kwa raha kwani alikufananisha na Jehanam lakini siku zilivyozidi kwenda alianza kuzoea,akapata mpaka marafiki.
Kitu kilichokuwa kinamtesa siku zote ni kazi ngumu kama kukata kuni na kubeba magogo,pamoja na yote hayo alijitahidi kujichanganya na wenzake.Kwa kufanya hivyo ilifanya apendwe karibia na wafungwa wote kwani hakuwa na makuu.Jambo lililokuwa linamuumiza kila siku ni mfungwa ambaye alionekana kuwa mzee sana na amekonda kupita kiasi,kichwani ana mvi nyingi.
“Lazima nijaribu kumdadisi”
Deo alitaka kujua sababu tangu awe mfungwa hakuwahi kumuona mzee huyo anakaa na wenzake mbali na hapo muda wote alionekana akiwa mwenye mawazo sana.Siku moja Deo alijitosa na kumuendea mpaka kwenye kona ya mwisho akiwa na chakula mkononi mwake.
“Shikamoo mzee wangu”
Deo akasalimia lakini mzee huyo alibaki akimwangalia bila kujibu chochote kile.
“Mimi naitwa Deo Karekezi”
“Mzee shikamoo”
Babu huyo hakuitikia alibaki akimwangalia Deo kwa kitambo kidogo!
“Marahabaaa mwanangu”
Mdomo wake haukuwa na meno yaani alikuwa kibogoyo kuashiria kuwa alikuwa ni kikongwe.
Siku hiyo Deo alianza kumuongelesha ingawa babu huyo alionekana kutokuwa tayari kuzoeleka ndiyo maana hakuwa tayari kuzungumza kitu kingine zaidi.
Lakini Deo hakuishia hapo, kila siku ilikuwa baada ya kufanya kazi nzito humfuata mzee huyo ambaye alipewa fununu kuwa yupo hapo kwa kifungo cha maisha kwa kosa la kuwauwa watoto wake pamoja na mkewe,Deo alitamani sana kusikia hadithi hiyo kinagaubaga.
“Niliuwa watotoo ndiyoo”
Babu alielezea kwa tabu kidogo kutokana na uzee aliokuwa nao.
“Kwanini babu?”
“Niligundua sio wangu,nikachukuwa bastola nikawapiga risasi walikuwa wanne.Baada ya hapo nikamuuwa na mke wangu”
“Pole sana,Kwanini ulichukuwa maamuzi kama hayo?”
“Ni hasira mpaka sasa hivi najutia mwanangu,nipo kifungoniii koho koho”
Mzee akakohoa kidogo na kumuangalia Deo.
“Nipo hapa tangu nina miaka thelathini na tisa,leo nina miaka tisini na mbili”
Siku hiyo Babu Magugu aliongea vitu vingi sana kuhusiana na maisha yake na alionekana kujuta kwa kitendo alichokifanya na kuanzia siku hiyo akawa rafiki mkubwa sana wa Deo.
“Kabla ya kutoka huku mjukuu wangu au Mwanangu,naomba nitafute kuna jambo nataka nikueleze.Usisahau”
Siku hiyo Mzee Magugu alimwambia Deo jambo hilo.
*******
Marietha,alipagawishwa vibaya sana na Penzi la Michael Muganda,akawa asikii kitu na aambiwi chochote kile kifupi alikuwa kama amepigwa sindano ya ganzi kwani hakusikia chochote kile.Akawa kama teja wa penzi na ilikuwa kila siku ni lazima jioni baada ya kutoka kazini wakutane na Michael wafanye ngono,hiyo ilimfanya Marietha asahau kabisa kama kuna mwanaume anaitwa Deo Karekezi,wakati mwingine alihisi kujuta kuwa naye kwani Michael Kwake alikuwa kila kitu.
“Hao watoto baba yao yuko wapi?”
Siku hiyo Michael aliuliza swali kwani alitaka kujuwa ni wapi baba wa watoto wake alipo.
“Naomba usinikumbushe kabisa”
“Kwanini?”
“Alifariki muda sana”
Mwanamke huyu sijui alikuwa ana matatizo gani,aliongea uwongo sababu hakutaka maswali mengine zaidi.Alihisi kumpenda sana Michael na aliamini kivyovyote vile hakuna hata mtu mmoja ambaye angeweza kuwatenganisha.Wakati mwingine alikufuru na kumuombea Deo afe hukohuko gerezani ili yeye azidi kutanua na Michael.
“Pole sana,leo dada yangu atakuja nataka nikutambulishe kwake”
“Mh,mimi naogopa”
“Sasa unaogopa nini mpenzi wangu?”
“Naona aibu”
“Usiogope yuko poa sana”
“Saa ngapi?”
“Leo jioni”
Maongezi hayo yalifanyika wakiwa juu ya kitanda,kichwa cha Marietha kipo kifuani kwa Michael Muganda na alikuwa akiongea akiwa amelegea mno.
Bila kusema kingine chochote kile akaanza kushika ndizi ya Michael ambapo hapohapo ikaanza kutuna na kukakamaa taratibu kisha ikasimama kama msumari,Marietha akashuka kidogo na kuiweka mdomoni akawa analamba kama koni.Mambo yaliendelea na wakati akiwa anafanya hayo yote mkono wa Michael ulikuwa juu ya chuchu zake,hiyo ilimpandisha midadi ikapelekea mpaka akaanza kuyafumba macho yake!Akamuendea Michael Midomoni na kuomba denda,raha alizopata hazikuwa rahisi kuelezeka,ndiyo maana alishindwa hata kusema chochote akabaki anatoa miguno tu ya puani.Michael akamchukuwa na kumkunja vizuri kitandani,akatumbukiza ndizi yake ndani ya mgodi.Kilichofuata hapo zilikuwa ni sauti za kitanda kunesa!
*****
Kama walivyohaidiana siku hiyo jioni, ilikuwa ni lazima Marietha aende kumuona dada yake na Michael.
“Dada yangu anaitwa Esta,ana macho makubwa kiasi kama yako”
Michael alianza kumpamba dada yake.
“Usimuogope,she is very okay sio muongeaji sana”
“Mimi nitaona aibu”
“Usijali”
Marietha alivyomaliza kujiandaa,wakatoka nje ambapo huko walichukuwa pikipiki mpaka kwenye hotel nzuri kiasi yenye viti vizuri na mapambo mazuri iliyopambwa na miti mizuri ya kuvutia.
“Ndio kafikia hapa,ametokea India leo.Itabidi nimpige kibomu anipe pesa kidogo na anco naye baadaye kaniambia nimtumie mahitaji ya chuo,nitampiga mzinga ili tukale bata baby ”
“Anafanya kazi gani dada yako?”
“Ni mfanya biashara,muwekezaji.Mbona Dar es salaam na Morogoro wanamfahamu sana!Keshawahi kununua hisa za Bakhresa,kipindi kile katoa unga wa Azam.Alikuwa ana hisa zake pale”
Michael aliendelea kupamba akatoa simu ya mkononi na kumtafuta dada yake hewani,alivyompata akamtaarifu kuwa yupo nje tayari.Aikuchukuwa dakika hata mbili,mwanamke mwenye rangi ya maji ya kunde,urefu wa wastani, mnene,mwenye macho makubwa akatokeza.Michael akasimama na kumuendea akampa mkono na kumsalimia,akampeleka mpaka meza aliyokuwa amekaa Marietha.
Ester Muganda alimuangalia Marietha kwa macho yasiyokuwa ya kawaida kwani sura yake haikuwa ngeni machoni mwake,Sura ya mfanyabiashara anayeitwa Deo Karekezi ikamjia hapohapo kichwani na alikumbuka vizuri sana siku ya harusi ya Deo na Marietha jijini Dar es salaam.
“Mariethaaa Karekezi”
Hapohapo Ester akaropoka akiwa na mshangao usoni,hiyo ilimfanya Marietha apagawe zaidi.

“Kwani mnafahamiana?”
Michael alimtupia swali dada yake huku akimuangalia usoni,alitaka kujuwa kama wanajuana na kama ndiyo hivyo walifahamiana wapi,alikuwa mwenye mengi ya kuuliza baada ya swali hilo.
“Huyu,namfahamu kuna rafiki yangu mmoja anaitwa Janeth Peter,anapenda kujiita Janeth Peter Bebe.Nimemfahamu kupitia yeye,tuachane na hayo.Mmesikilizwa?Alafu hujaniambia Michael ndiyo wifi nini?”
Ester Muganda ni mwanamke mdogo lakini alikuwa mjanja na hakuwa na tabia ya kufuatilia watu,ndiyo maana alizuga sababu picha aliyoiona ilimfanya ashindwe kuropoka chochote kwani hakutaka kuharibu,hiyo ilimshangaza sana Marietha lakini hata hivyo alitabasamu na moyo wake ulihisi kumkubali sana Ester Muganda,ndiyo maana akamchangamkia na kuweka tabasamu mwanana usoni.
“Ndiyo wifi yako huyu,mzuri eeh?”
Michael akaanza kuuliza akihitaji Marietha asifiwe.
“Hiko ni kifaa mdogo wangu,fanya umlete nyumbani mara moja”
“Sema kweli”
“Sina utani na wewe,My wii ana macho mazuri sana”
Hiyo ilimfanya Marietha atabasamu tena na kufurahi kwa ujumla,hapo waliendelea kunywa na baadaye chakula kikaletwa.Maisha kwa Marietha tangu awe na Michael kimapenzi yalikuwa ya raha mustarehe,akasahau kila kitu kilichopita nyuma, wakati mwingine alijuta kuolewa na Deo na kichwani kwake alitawala Michael tu.
“Agiza Savvana Marietha”
“Hapana mimi sinywi”
“Moja tu”
Michael alitumia ushawishi mkubwa sana,hatimaye Marietha akakubali kuagiza pombe hiyo inayoitwa Savana.
‘NJOO PEMBENI TUONGEE’
Ulikuwa ni ujumbe uliosomeka juu ya kioo cha simu cha Ester Muganda lakini alikuwa amemuwekea Michael mbele yake.
“0na meseji ya Mama anavyosema,ngoja nikuonyeshe nyingine”
Ester akatumia ujanja mwingine,akaandika meseji kwenye simu yake na kumuwekea simu tena mbele yake lakini Marietha hakuona ujumbe huo.
‘SASA HIVI NJOO TUONGEE KUNA KITU NATAKA KUKWAMBIA’
“Mama anataka kupiga,anasumbua sana.Njoo pembeni”Ester akasema tena.
“Poa,twende basi pembeni hapa kuna kelele”
Huo ndio ujanja waliotumia mtu na mdogo wake kumtoka Marietha kwenda chemba bila yeye kujua.Wakatoka mpaka nje kabisa ya eneo la hoteli hiyo na kuzunguka nyuma ya geti.
“Michael nisikilize mdogo wangu kwa makini,huyo ni mke wa mtu.Kuwa makini,nakwambia kuwa makini”
Ester aliongea kwa msisitizo huku akimuangalia mdogo wake machoni,alielewa nini maana ya kutembea na mke wa mtu,ndiyo maana alimkanya mdogo wake asifanye hivyo kwani mwisho wake ungekuwa mbaya sana.
“Ndio najua lakini mumewe alifariki ameniambia”
“Amefarikiii?Amefariki lini?Muongo, mimi namfahamu huyu Marietha mumewe namjua, sikukatazi kuwa naye lakini uwe makini,usionekane naye hovyo mdogo wangu.Mimi dada yako,tupo wawili tu”
“Sawa dada nitakuwa makini mume wake kwani yuko wapi?”
“Sijui alipo lakini ni mfanyabiashara”
“Yupo hai?”
“Hilo mimi sina uhakika Mike”
“Aya sawa sista lakini mimi sina kitu sasa hivi.Nilinde basi si unajua nipo na mamaa pale”
“Usijali,Anco Mtui hajambo?”
“Mzima yeye”
“Nitaenda kumuona mwezi ujao,bado nipo bize bize kidogo”
Swala hilo la Marietha kwamba ni mke wa mtu lilimuingia Michael kichwani na kurudi mpaka kwenye meza waliomuacha Marietha.
“Uliboreka eeh?”
“Hapana usijali”
Michael,Ester pamoja na Marietha waliendelea kunywa na ilivyofika mishale ya saa saba usiku kila mtu alitawanyika.
“Twende tukalale lodge leo”
Michael alitoa pendekezo wakiwa njiani wanatembea,Marietha akalipitisha na hapohapo wakaanza kuangaza huku na kule kutafuta vibao vya matangazo.Haikuchukuwa muda mrefu wakafanikiwa kuona kibao kilichoandikwa Mzizima Lodge(Self contained)Nyumba hiyo ya wageni ilimaanisha kuwa ndani kuna kila kitu,hakukuwa na muda wa kupoteza wakaanza kunyoosha kukifuata kibao kilichokuwa upande wao wa kushoto.Kwa kuwa Michael alikuwa ana pesa alizopewa na dada yake mfukoni,haikuwa kazi ngumu na hata kama angelala humo kwa siku mbili nzima pesa ingetosha,walipata chumba kizuri chenye kitanda kikubwa na bafu zuri.Baada ya kufunga mlango, Michael alimsogelea Marietha mdomoni akatoa ulimi wake,ukadakwa kinywani kwa Marietha akaanza kuuzungusha.Hisia zao tayari zilihama na kila mtu alisisimka mwili kiasi kwamba hawakuweza kufikiria kitu kingine zaidi ya kufanya ngono na hicho ndicho kilichowafanya mpaka wakodi chumba.Marietha alianza kurudi kinyumenyume niya yake ikiwa ni kujitupa kitandani,na hivyo ndivyo ilivyokuwa kwani alijitupa kitandani na kulala chali,Michael akasogea na kumpandia juu yake akiendelea kumnyonya mdomo,akapitisha mkono wake taratibu mpaka nyuma ya sketi aliyovaa akashusha zipu,akaanza kuvuta sketi,Marietha akajiinua kidogo kwa juu na kunyoosha miguu yake,sketi ikatoka akabaki na chupi peke yake.Hiyo ilimfanya Michael pia apitishe pia mkono nyuma ya mgongo wa Marietha na kufungua zipu,blauzi ikatoka,akabaki na sidiria peke yake.Kwa Michael kutoa blazia ya Marietha ulikuwa mtihani kwani iligoma kutoka hiyo ilifanya mpaka Marietha ainue mgongo na kuivua mwenyewe,ikaachia na kilichoonekana yalikuwa ni maziwa.Michael hakuchelewa, hapohapo aliyafakamia na kuanza kuyanyonya, hiyo ilimfanya Marietha ayafumbe macho yake kwani alichokihisi kilishindwa kuelezeka kiwepesi.
Kulikuwa kuna kama wadudu wa utitiri wanatembea ndani ya damu yake,alihisi kuchanganyikiwa zaidi baada ya mkono mmoja wa Michael kuingia ndani ya chupi na mgodi wake kuanza kutomaswa,akahisi kama ameota mbawa anapaa angani.
“Aaaah aaaaaah”
Marietha aliguna huku akisikilizia jinsi chupi yake inavyovuliwa,akahisi kama amepigwa sindano ya ganzi baada ya shingo yake kuanza kunyonywa alipochanganyikiwa zaidi ni pale ulimi wa Michael ulipogusa mgodi wake,hiyo ndiyo ilifanya mpaka aanze kutoa mihemo ya juujuu huku akiwa anakishika kichwa cha Michael akikikandamiza kabisa ndani ya mgodi wake.
“Aaah Mich…ael li..ke th..at usiiacheee aah aah aah aah aah aaah,usiacheee”
Marietha alilalamika huku akitoa sauti za puani,namna ambavyo Michael alimfanya ilifanya mpaka aanze kukinyonga kiuno kwani alihisi anakaribia kufika mshindo,ndiyo maana akaanza kuyavuta vuta mashuka na kujinyonga kama nyoka aliyemwagiwa mafuta ya taa!
*******
Marietha na Michael walimaliza kuzini saa kumi kasoro za asubuhi na kila mtu alikuwa hoi bin taaban,kwa Marietha ndiyo usiseme kwani aliweza kwenda mizunguko kumi na mbili kwa masaa machache, jambo ambalo alilichukulia kama miujiza na kifupi Michael alivunja rekodi,bado alikuwa kitandani anatafakari na kujiuliza kwanini hakujuana na Michael mapema.
“Baby nime enjoy sana”
Marietha alianza kumwaga sifa.
“Hata mimi.Umenifanya niende kasi sio siri”
“Wewe hapo bwanaaaa”
“Lazima nikusifie.Siku zote usijisifu kwa mbio msifu na anayekukimbiza”
Wakati wanaongea hayo Marietha alikuwa kifuani mwa Michael anamkwaruza na kucha kimahaba,hiyo ilifanya ndizi ya Michael taratibu ianze kutuna hatimaye ikaanza kuwa ngumu mishipa ya pembeni ikawa nganganga,Marietha alivyoona hivyo alijuwa nini anachotakiwa kufanya kama mwanamke aliyekamilika kila idara,akasogea kidogo kwa chini na kuitumbukiza mdomoni.
Alivyoona hapati nafasi nzuri akasogea tena karibu,akawa amelalia tumbo,hapo ndipo alipoanza kulamba ndizi ya Michael kwa fujo kana kwamba alifungwa mota,Moto wa Michael ulianza kupanda hapohapo akaona isiwe tabu,akamsogeza kando na kumtoa kutoka kitandani.
“Inama kidogo,shika magoti”
Michael aliongea sentensi nne tu,Marietha akawa kama mwanakondoo akatii akainama nyuma Michael akasimama kama ngongoti,akachukuwa ndizi yake vizuri na kuitumbukiza ndani ya mgodi.
“Paaaaa”
Kibao cha makalio kilisikika, huyu ni Michael ndiye aliyempiga Marietha kwenye makalio huku akianza kunyonga kiuno chake,kasi ilikuwa kubwa hiyo ilifanya mpaka Marietha ashindwe kupata stamina za miguu,akaweka mikono yake ukutani ili apate balansi.Mtanange uliendelea na Michael alifanya kila njia kupenyeza ndizi yake kila kona ya mgodi.Alivyohisi anafika mshindo alimvuta kitandani na kumbwaga puu,akapanda juu yake na kuingiza ndizi taratibu huku akichukuwa mguu mmoja wa Marietha na kuuweka begani.Utamu ulizidi kukolea kadri Michael alivyozidi kuongeza kasi!
“Aaaah aaah aaaah”
Marietha alitoa sauti za puani.
“Baby,I’m cumming aaah aaah aaaah.Hivyo hivyoo..ooo”
Sauti ya Marietha ilikuwa ya juu hiyo ilifanya mpaka Michael azidi kukoroga kiuno chake na hazikupita hata sekunde nane akawa ametulia juu ya kifua cha Marietha,Sekunde hiyo hiyo Marietha akamkumbatia kwa nguvu kumaanisha kuwa wamefika kwa wakati mmoja ama wamepishana sekunde moja tu kama sio mbili.
*******
“Bosi nisamehee,sitorudia tena mwanangu alikuwa anaumwa nilienda hospitali”
“Marietha haiwezekani.Kwanini usitoe taarifa kwani hauna simu?”
“Ninayo bosi”
“Sasa kwanini hukutoa taarifa kuwa mwanao anaumwa?Kwani sisi hatuna watoto?Alafu siku mbili tatu hizi umebadilika sana.Unatoka kazini mapema,hupiki chakula kikaiva vizuri.Juzi niliambiwa umeunguza chakula”
“Bosi nisamehee”
“Subiri,usikimbilie kuomba msamahaa.Unajua mteja mmoja kula chakula kibovu tunakuwa tumepoteza wateja zaidi ya mia moja.Unalijua hilo?”
“Ndio bosi naelewa,sitorudia tena”
“Hapana,hauna kazi.Nenda kapumzike kwanza”
Marietha alidondoka kwa magoti na kutembea mpaka kwenye meza ya meneja Martin Nguzu,mwanaume aliyekuwa kauzu kuliko dagaa na hakuwa na mchezo katika kazi yake.
Historia yake ilikuwa mbaya na hakuwahi kumsaheme mfanyakazi yoyote yule.Hiyo ilifanya mkurugenzi wa hotel hiyo ampandishe mshahara kutokana na kupiga kazi na usimamizi mzuri.
“Usinipigie magoti Marietha,mimi sio Mungu wako.Toka ofisini kwangu kabla sijaita walinzi”
Martin Nguzu alizungumza kwa kufoka kidogo,jambo alilofanya Marietha lilimkera kilichomchefua zaidi ni tabia alizoanza Marietha za kuwahi kutoka kazini lakini alichokasirika zaidi ni baada ya siku hiyo ya Jumatatu kufika saa saba ya mchana.
“Unakuja saa hizi?Hii hoteli ya baba yako?Nakuuliza hii hoteli ya baba yako?Toka ofisini kwangu”
“Bosi,nisame…he sitorudi te..na ni..po tayari unikate pe..sa kwenye mshahara wan..gu lakini usinifukuze ka..zi ndi..yo nayotege..mea ukoo mzi..ma unani..tegemea mwa..nangu anaumwa amelazwa nionee huruma bosi..Nionee huruma,naomba msamaha.Nilichanganyikiwa ndiy..o maana sikupiga si..mu”
Katika kuigiza Marietha alikuwa hodari na hakuelewa siku hiyo machozi aliyatoa wapi sababu aliyakamua mililita kumi nzima,akatoa mpaka kamasi akiwa amepiga magoti.Kufukuzwa kazi katika hoteli hiyo ilikuwa ni sawa na kutoswa jangwani sababu hakuwa na cheti kwani hakwenda shule.Hiyo ilimfanya Mr.Martin Ngusa amuangalie Marietha kwa huruma sana,hasira zake zikashuka kiasi kwani kwake kupigiwa magoti lilikuwa jambo kubwa sana katika maisha yake.
“Nimemuonea huruma huyo mwanao,sio wewe.Kaendelee na kazi.Lakini next time sitaki huo uzembe ujitokez!UNDERSTOOD?”
Martin Nguzu akaongea kwa ukali kidogo na sura yake ilikuwa siriazi,hiyo ilimfanya Marietha asimame na kuitikia kwa adabu zote,mikono nyuma! Akapangusa magoti yake michanga na kutoka nje ambapo huko aliendelea na kazi kama kawaida.
*********

Kukosa penzi la Michael ilimpelekea mpaka apate ugonjwa mbaya wa arosto,kompyuta ya kichwani kwake haikuweza kufanya kazi kabisa, hiyo ilimfanya mpaka ahangaike huku na kule na akipata nafasi ilikuwa ni lazima aifanyie kazi ipasavyo.Penzi lake na Michael liliendelea na alijihisi kama amekamilika hiyo ilifanya mpaka awasahau watoto wake,hakuwapa malezi yanayotakiwa na wakati mwingine aliwaacha na njaa na kukesha baa akijivinjari na Michael,alijuwa kwa kufanya hivyo anafanya makosa lakini hakujali.
Aliendelea kula bata na kufanya starehe,pesa alizopata hakupeleka tena benki kuhifadhi ama kuweka akiba bali alizitumbua na Michael kwenye hoteli mbalimbali za gharama.
“Chuo nafungua wiki ijayo mpenzi wangu”
Michael siku hiyo alimwambia Marietha.
“Baby nitakumisi sana.Sitoweza kukaa mbali na wewe”
“Itabidi uzoee”
“Itabidi twende wote Darling”
“Na kazi?”
“Niachie mimi,nitaandika barua ya likizo”
“Hapo sawa,wewe kiboko”
Hayo ndiyo yalikuwa makubaliano ya Marietha, na kuanzia siku iliyofuata alianza kuandika barua ya likizo akisingizia kuwa mwanaye anaumwa hivyo anahitaji kukaa naye karibu.
Baada ya siku tatu akaipeleka katika uongozi wa Hoteli na kusubiri majibu ambapo ilijibiwa siku mbili baadaye kuwa amekubaliwa na amepewa likizo ya siku saba tu.

Kwake ilikuwa ni sherehe kubwa kwani aliamini huo ndiyo ulikuwa muda mrefu wakufanya matanuzi na kipenzi chake, Michael Muganda.
“Nitakuachia watoto hawa Rebeca,utanisaidia kukaa nao.Nikifika Dar nitakutumia pesa kidogo”
“Utarudi lini?”
“Kesho kutwa nadhani.Kuna mtu naenda kumuona ni muhimu sana, sasa siwezi kwenda na watoto”
“Sawa mimi sina shida ilimradi tu,utume hayo matumizi”
“Hilo halina shida,shukrani sana”
Kama mtoto wake Abraham angesikia Mama yake anaondoka habadani asingekubali kwani alimpenda sana na siku zote alilia kwa sauti kubwa kama Mama yake angekuwa mbali.
*****
Taratibu za safari zilianza mara moja na wiki moja baadaye Marietha na Michael wakawa wameingia, jijini Dar es salaam!

*******
ENDELEA KUSOMA HADITHI NA SIMULIZI ZA MTUNZI….EMMANUEL F.KWAY(THE STORY MASTER)

0 comments:

Post a Comment

BLOG