Search This Blog

Sunday, May 31, 2020

BEDROOM PROFESSIONALS SEHEMU YA 8/10



BEDROOM PROFESSIONALS
MTUNZI….EMMANUEL F.KWAY(THE STORY MASTER)
AGE…(18+)
WatsApp…+255718 862176
SEHEMU YA 8 KATI YA 10 MWISHO
*******

O.

Saa 2:30 mchana, ndipo Michael na Marietha waliingia jijini Dar es salaam na kitendo cha kufika
Ubungo hawakutaka kupoteza wakati wala kuuliza chochote bali walikodi Bajaji na safari ya kwenda Ubungo ‘riverside’ kuanza,huko ndipo Michael alipopanga chumba kimoja kama ‘hostel’ ya kuishi akiwa anasoma chuo kikuu cha Dar es salaam (UDSM).
Ilikuwa ni shangwe kwa Marietha kufika salama na uchungu kwa wakati mmoja kwani jiji la Dar es salaam,lilimkumbusha vitu vingi sana.Ingawa alijaribu kujizuia visipite ndani ya ubongo wake lakini ilishindikana.
“Kwa Mlacha kaka,huko unatupeleka wapi tena kiongozi?”
Michael alivunja ukimnya, baada ya kuona bajaji inapita njia ambazo hazielewi,kutoka stendi ya Riverside mpaka kwa Mlacha ulikuwa ni mwendo wa dakika arobaini na tano na sio kwamba palikuwa mbali bali ni barabara mbovu, hiyo ilifanya magari yatembee mwendo wa kinyonga.Alichofanya dereva wa bajaji ni kutaka kutumia njia nyingine aliyoamini kuwa itakuwa rahisi kwake kwani hakutaka kukiingiza chombo chake kwenye makorongo!
“Broo,huko hakupitiki”
“Kuna nini?”
“Kule mbele barabara mbovu sana juzi mvua zilinyesha.Nataka kupitia huku kibangu”
“Poa”
Maelezo ya Dereva yalifanya Michael atulie na kumuangalia Marietha ambaye alionekana yupo mbali kimawazo.
“Darling,karibu Dar es salaam”
“Ahsante nishakaribia”
“Hivi ushawahi kufika Dar es salaam?”
“Yeah,sema niliondoka muda sana naona mji umebadilika kidogo”
“Ni kweli,mambo yanaenda harakaharaka sana.Huku zamani kulikuwa ni msitu mkubwa sana.Sasa hivi, watu wanajenga majumba,muda si mrefu kutakuwa mjini”
“Ni kweli,mji unakuwa ndio vizuri lakini”
Bajaji ilizidi kusonga mbele huku ikiyumba yumba kutokana na makorongo na barabara kuwa mbaya ya kutisha.
“Simama hapo mbele kidogo”
Michael akamwambia dereva wa bajaji kwani tayari alikuwa amefika,wakampa ujira wake kisha wote kuteremka.Hukukuwa na mtu yoyote kati yao aliyekuwa na mizigo mikubwa kwani Marietha alikuwa ana mkoba na Michael alikuwa ana begi dogo la mgongoni.
Wakatembea kwa miguu na kuingia kichochoro kidogo,ambapo baada ya hatua kumi na sita Michael aliingiza mkono mfukoni na kutoa funguo za kitasa cha mlango kumaanisha kuwa wanakaribia kufika.Ni kweli sababu mbele kidogo waliingia ndani ya nyumba kubwa na ndefu kiasi,wakapita katikati ya korido na kuvipita vyumba vingine,wakasimama nje ya mlango wa tatu kutoka mlango mkubwa.
“Karibu geto”
“Ahsante”
Michael akafungua mlango,kilikuwa ni chumba kidogo lakini kisafi mno.Kapeti zuri.Televisheni kubwa ‘flat screen’ nchi 48.Kitanda kilikuwa kikubwa na pembeni kidogo kulikuwa na vyombo,kushoto jiko la gesi,kulia friji dogo la LG.Kilikuwa ni chumba finyu lakini kizuri kutokana na jinsi ambavyo kimepambwa na vitu vya kisasa!
“Kwako pazuri,nimepapenda kwa kweli”
“Kuzuri wapi.Hapa nataka kuhama,padogo sana”
“Sipati picha unavyoingiza mademu humu”
“Ah wapi,mimi kauzu.Humu aingii demu yoyote yule wewe wa kwanza”
“Michael acha uongo”
“Nakwambia ukweli”
“Babra yuko wapi siku hizi?”
“Hivi unadhani yule alikuwa demu wangu basi”
“Kumbe?”
“Tuachane na hayo,nitakwambia siku nyingine”
“No Michael,mimi moyo wangu ni mwepesi kuumia.Tafadhali naomba usiniumize nakupenda sana.Nimeamua kuwa nawewe,nitunzie moyo wangu”
“Hilo pigia mstari”
Kazi ya Marietha siku hiyo ilikuwa ni kufuta vumbi la hapa na pale, kutokana na chumba hiko kukaa kwa muda mrefu bila kuguswa,baada ya hapo aliingia bafuni kuoga na alivyotoka alijitupa kitandani na kuchukuwa simu yake.
“Baby nakuja,ngoja niende hapo nje kucheki chakuka tupike nina njaa sana”
“Poa love,mimi nakusubiri”
“Washa t.v”
“Nitawasha usijali ngoja nipumzike”
Kifupi Moyo wa Marietha ulikuwa mweupe na aliridhia kuwa na Michael kwa hali yoyote ile na wakati mwingine alitamani hata aache kazi na kuendelea kubaki na Michael kipenzi cha roho yake,hivyo ndivyo mtima wake ulimwambia ufanye na aliuheshimu sababu aliogopa kuumia!
Michael alivyorudi, alikuwa na vyakula mkononi tayari katoka kununua kumaanisha kuwa kinatakiwa kupikwa,akapita moja kwa moja mpaka kwenye jiko la gesi.
“Unataka kufanya nini?”
Marietha akauliza akiwa kitandani na kanga moja peke yake,mapaja yote yapo wazi.
“Nataka nipike tule”
“Kaa pembeni sweatheart mimi nitapika”
“Baby usijali”
“Michael please kaa pembeni acha nipike,yaani wewe upike mimi nipo umeona wapi”
Hapohapo Marietha akatoka kitandani na kusimama,akaandaa kila kitu kama kuchambua mchele kukata kata nyama na vitunguu pamoja na nyanya kisha kuweka kila kitu jikoni.Alifanya hivyo kutokana na penzi alilokuwa nalo ndani ya moyo wake,sio siri hakuelewa ni kivipi mwanaume huyo kamwingia kwa haraka ndani ya moyo wake.Ndani ya dakika arobaini na saba chakula kilikuwa tayari kimekwiva na wote wakaanza kula.Sio siri chakula kilikuwa kitamu kwani Michael alikisifia na kudiriki kusema kuwa hakuwahi kula chakula kitamu namna hiyo.
“Wewe ni fundi baby”
Michael aliendelea kumwaga sifa kedekede,chakula alichokula kilifanya ashibe ndindindi.
“Maji Honey”
Ni Marietha ndiye aliyemimina maji na kumkabidhi Michael,siku hiyo Michael alijifananisha na baba mwenye nyumba na Marietha ni mkewe.Alijisikia furaha na amani ndani ya moyo wake,kitendo cha kuweka glasi chini.Michael akatembea na kufunga mapazia,akatembea mpaka kweye ‘sub woofer’ yaani redio yake kubwa akaweka mziki mkubwa kiasi,alichokuwa anataka kukifanya anakijuwa mwenyewe kwani aliongeza tena sauti ya juu kiasi.
“Baby let me put your panties to the side.I’mma make you feel alright.Cause I’mma give you what you need yaaah”
Hiyo ndiyo nyimbo ya kwanza kupigwa kwa sauti kubwa kiasi,Michael akaanza kucheza kidogo.Alimpenda sana Chriss Brown ndiyo maana hata ukutani kulijaa picha za mwanamuziki huyo wa kimarekani.
“Hii nyimbo naipenda sana,na inahusu tukio tunaloenda kufanya”
Michael akaanza kuongea taratibu huku akisogea karibu ya kitanda akivua shati lake.
“Anasema, mpenzi nataka kuweka chupi yako pembeni.Nataka kukufanya ujihisi vizuri kwani nitakupa kile unachotaka nyimbo inaitwa Show me, kashirikishwa na kid inc”
Kumalizia hapo akawa tayari keshafika kitandani,akamfuata Marietha mdomoni na kumpa ulimi,ukadakwa wakaanza kulana madenda na kunyonyana ndimi huku mziki taratibu ukiwa unarindima, niya Michael kuweka mziki ilikuwa ni kufanya sauti ya miguno isitoke nje kwani kulikuwa na majirani wengine nje.
Sio siri Marietha alibarikiwa kuwa na mapaja menene na malaini na hayo ndiyo Michael alikuwa akiyatomasa huku akiwa mdomoni ananyonya midomo ya mwanamke huyu mrembo sana aliyekuwa mtamu kuliko asali,kwa Marietha alikuwa amevaa kanga peke yake,haikuwa tabu kwake kuupitisha mkono juu ya chupi na kuanza kushika ikulu taratibu,alivyoona haitoshi akaingiza mkono kwa ndani kabisa na kuendelea kupapasa mgodi ambapo alitumia pia kidole kimoja kuchimba madini,mambo yalikuwa mukidemukide kwani damu ya Marietha ilianza kuchemka vibaya sana,akatoa mkono wake na kushika ndizi ya Michael iliyokuwa tayari imesimama dede,akili yake ilihama kabisa kwani raha alizohisi hazikuwa na mfano wake.Bila kujijua akapinduliwa na kuwekwa vizuri,chupi yake ikatolewa,ulimi wa Michael ukawa juu ya chuchu zake nyeusi hapo ndipo alipohisi kufa kufa,akaona kama anasimama na kucha moja ya mguu.Kitu kilichompagawisha zaidi ni pale ndizi ya Michael ilipokuwa inazama taratibu ndani ya mgodi wake,inatoka na kuingia tena taratibu.
“Ashiiiii ashiiiiiii”
Marietha alikuwa akiguna na kusikilizia mambo yanavyoenda na kadri sekunde zilivyozidi kwenda ndipo alipozidi kuhisi raha zaidi na zaidi.
“Kaa hivii”
Michael alitoa agizo na kuchomoa ndizi yake jambo ambalo lilimkera kiasi Marietha ambaye tayari alikuwa mwenye moto, hakuwa na jinsi alitii amri na kupewa maelekezo kuwa alalie tumbo kisha ajibinue kwa juu,hapohapo Michael akaingia juu yake.Mambo yaliyoendelea hapo yalifanya mpaka Marietha azidi kupiga kelele,kila mkao ulibadilishwa na baada ya dakika kama tano hivi wakawa teyari wamefika mshindo,wakapumzika kidogo kwani walikuwa bado wana uchovu wa safari.

********
Siku iliyofuata Michael alidamka asubuhi na mapema kwani ilitakiwa aende kuonana na mjomba wake Mtui, akachukuwe pesa za ada ya chuo na mahitaji mengine,alimuaga Marietha na kuondoka zake.Ilikuwa ni lazima kutoka kwa Mlacha mpaka barabarani uchukuwe pikipiki kwani daladala zilikuwa hadimu kupatikana hivyo ilimlazimu achukuwe pikipiki sababu alitaka kuwahi ili arudi abaki na Marietha wake.
Alivyofika stendi, akachukuwa daladala la Tegeta,dakika sitini na moja baadaye alikuwa amefika Tegeta Nyuki,akashuka na kuanza kupiga mguu,mpaka alipofika nyumba yenye geti la rangi nyeusi,akabinya kengele.Mlinzi wa kimasai akatoka.
“Aseeee Michael.Subuhi subuhi.Mimi sijui mwisi nilitoka na sime kuja kata…”
“Mzee yupo?”
Michael hakutaka kusikiliza stori za Masai kwani alikuwa mwenye maneno mengi sana ndiyo maana alimkatisha.
“Ipo,ipo pale aseeee”
Hakujibu tena kitu chochote,akaanza kutembea mpaka alipofikia mlango mkubwa akagonga kidogo na kunyonga kitasa akazama ndani,bahati nzuri alimkuta Mtui ndiyo yupo kwenye kochi anavaa viatu.
“Oh Michael,karibu”
“Ahsante shikamoo Anco”
“Marahaba,nilikusubiri kweli.Ndio nilikuwa nataka kutoka hivyo”
“Foleni anco,ndiyo maana umeona nimechelewa”
“Ile karatasi unayo?”
“Ndiyo ninayo”
“Embu nipatie”
Mahitaji ya chuo,kuanzia karo,kodi ya pango,pesa ya chakula vilikuwa juu ya karatasi na hivyo vyote Michael alikuwa ameviorodhesha na kuongeza sifuri kadhaa mbele.
“Kwahiyo total ni milioni nne na hamsini?”
Mtui akauliza huku akiangalia karatasi vizuri kisha kumtizama Michael usoni.
“Ndio Anco”
“Mbona imezidi namna hii?”
“Yule mzee kapandisha kodi,alafu kule nilipopanga ni mbali kidogo na chuo”
“Tuition fee pia imepanda?”
“Ndio anco”
“Alafu nalipa tu ada,sipati matokeo yako ya chuo.Last semester ulikuwa na G.P.A ya ngapi?”
“2.2”
“Bado bado bado kabisa.Next time jitahidi sana,nikienda ofisini leo nitakuingizia pesa kwenye akaunti yako nusu kwanza,nyingine wiki ijayo”
“Ahsante anco”
“Ujitahidi usome!Elimu siku hizi ndiyo kila kitu. Siku hizi hakuna tena kubeba zege kila kitu ni mitambo tu.Achana na mambo ya kampani mbovu hazina inshu”
“Nitajitahidi anco”
Moyo wa Michael,ulijawa na furaha kwani alijuwa siku hiyo anaenda kupiga pesa ndefu kwani milioni nzima alikuwa ameweka cha juu.Alirudi geto kwa Mlacha na kukuta Marietha ameshaandaa chakula cha mchana,akampasha habari juu ya mkwanja alioupata kwa mjomba wake.Jioni ilivyofika alivyoenda kuangalia salio benki akakenua meno kwani akaunti ilisoma pesa na ilikuwa lazima usiku huo waende disco kuruka majoka kutumbua pesa za mjomba wake.
*******
Maisha ya Marietha kuanzia alivyofika mjini yalikuwa ni kuruka majoka usiku,akawa kama popo usiku halali,kila club aliijua na alijirusha kisawasawa na kujiachia na Michael.Bata alilokuwa anakula na Michael halikuwa la kawaida kabisa,hiyo ilifanya ajione yeye ndio yeye hakuna hata mtu mmoja aliyembana na walifanya ngono popote pale walipojisikia.Kwa kuwa Michael alikuwa ana pesa, siku moja aliamua kuwaalika marafiki zake ‘night club’ inayoitwa Mikasa na siku hiyo ndiyo ilikuwa kufuru kwani kila mtu alikuwa na mpenzi wake pembeni,bado walikuwa wanafunzi na wazazi wao wanajuwa wapo hostel wanajisomea.
“Weka mbili mbili.Marietha mpenzi wangu,maishaa mafupiii sana.Lets pariiiiiiiiii”
Michael akapiga kelele na kusimama katikati ya marafiki zake,akionesha umwamba na kujitapa kuwa yeye ndiye tajiri, akamvuta Marietha na kumnyonya mdomo, yaani denda.

Siku hiyo ilikuwa Ijumaa na siku zote Mtui hupenda sana kutoka usiku wa saa tatu kwenda kupumzika sehemu nyingi tofauti tofauti,yeye na marafiki zake walichagua sehemu inayoitwa Mikasa pia walitaka kuingia ‘night club’ ili wanywe mbili tatu kisha wahame kijiwe!
“Angekuwepo Deoo hapa,ninge enjoy sana.Maaana yule jamaa mtafutaji alafu sio bahili,ana mahesabuuu ya pesaa”
Mtui alimwambia rafiki yake baada ya kufika kaunta na kukaa viti virefu.
“Deoo?Deo yupi huyo?”
“Yule rafiki yangu yupo gerezani nimekwambiaaa Kakone, tatizo kichwa chako hiko kinashindwa kunasa vizuri.Juzi juzi hapa si nilikwambia ku…”
“Basi basi yaishe nina kiu.Dada embu nipe Heinken mbili hapa,msikilize na rafiki yangu,kwenye bili yangu weka”
“Hii sehemu sijaja siku nyingi sana.Pame change mnooo,mara ya mwisho nilikuja na Dokta Eruwaichi anakuunywaa pombee huyoo kama ana pipa tumboni”
“Wewe si umezoea kwenda baa zako za kizee.Hapa kwa wajanja Mikasa Mikasa”
“Acha maneno,wiki ijayo nitakupeleka kwa rafiki yangu fulani kafungua night club huko Temeke”
“Mambo yako ya kizee mimi nakujua,unaenda baa kama unaenda kwenye msibaa”
Pombe ziliwekwa mezani wakapiga ‘cheers’ na kuanza kupooza makoo yao.
Lakini katika kugeuka nyuma Mtui akaona kitu kilichomshangaza kupita kiasi,hiyo ilifanya mpaka apaliwe na bia.Hakuwa ana uhakika kama aliyemuona alikuwa ni Marietha akiwa katikati ya kundi la watu tena amevaa sketi ya kimini mapaja yote nje, ameshikiliwa kiuno na kijana ambaye hakuweza kumtambua vizuri kwani alikuwa amempa mgongo!Mtui akakaza macho na kuyafikicha ili aangalie vizuri.Hiyo ilifanya mpaka bwana Kakone ageuze shingo yake pia.
“Mtui vipi?Umemaindi mzigo nini?Hapa kuna watoto wakali lakini makahaba,ukijichanganya umeibiwa”
Kakone akauliza na kutia neno.Lakini Mtui hakujibu badala yake aliendelea kumkata jicho mwanamke aliyemfananisha na Marietha.
“No!”(Hapana)
Mtui alikema kwani aliyemuona alikuwa ni Marietha,sababu haikuwezekana hata kidogo watu kufanana namna hiyo.

**************
“Baby naenda chooni,nisubiri hapo”
Michael aliongea kwa sauti kubwa akimuaga Marietha, akamvuta tena karibu na mdomo wake,akamnyonya mdomo na kumbinya kalio.Hakuelewa kuwa mjomba wake Mtui pia yupo ndani ya Club hiyohiyo!
“Ommy,nilindie shemeji yako”Akaacha maagizo!
Mtui alishindwa kuvumilia, akatamani kumfuata mwanaume aliyekuwa na Marietha lakini akashindwa aanzie wapi,alichofanya yeye ni kuacha chupa yake ya bia na kuanza kutembea kuelekea kwenye makochi aliyokuwa amekaa Marietha na vijana wengine wakiwa wanavuta sigara na shisha!
“Mariethaaaaaa!”
Mtui akaita kwa sauti,Marietha akageuka moyo wake ukapiga paaa,akahisi kama amepigwa sindano ya ganzi mwilini!
“Mariethaaaaa,hivi kweli una….”
“Hivi unanitakia nini wewe mzeee?Si nilishakwambia sikutaki au?Mbona unanifuatilia fuatilia?”
Marietha aliongea kitu ambacho kilimfanya Mtui ashindwe kusema kitu kwani alizungumza habari za ajabu siku hiyo, niya yake ikiwa ni kumziba mdomo asiseme habari za Deo hiyo ilifanya kijana mmoja aliyekuwa pembeni anavuta sigara na shisha,asimame.
“Mzee vipi?Kavu nini?Sanzuka bwanaaa.Hivi vizeee vipi?”
“Kijana,embu toka mbele yangu.Usije ukatafuta shida baadaye,sogea mbele yanguu”
“Mzee umerogwaa nini…Oyaa Chale,embu tumfanyizie huyu mku****”
“Kijana,toka mbele yangu”
“Mzee mse**** nini.Sepa bwanaaa”
Kijana mmoja akasimama na kuingilia ugomvi huo,Mtui akawa amezungukwa na watu wanne na ilielekea walitaka kumpiga na kumfanyia fujo kwani jinsi walivyomuangalia ilitishia amani hata yeye aliogopa,hiyo ilifanya Mtui ashike kiuno chake na kukamata bastola vizuri,akasogeza shati kidogo huku akiwatizama machoni kwa hasira.
Ilibidi vijana waliojifanya mabondia waanze kurudi kinyumenyume kwani waliona bastola kiunoni mwake.Kabla ya kukaa sawa Michael akatokeza hapohapo,moyo wake ulipiga kwa nguvu baada ya kumuona mjomba wake Mtui amesimama.
Hiyo ilikuwa wazi kabisa siku hiyo ndiyo ingekuwa mwisho wa elimu yake kwani Mtui alimuonya sio chini ya mara moja, kuhusiana na tabia zake za kulewa pombe na kufanya starehe.
“Baby tuondoke sasa hivi”
Marietha ndipo alipoharibu kabisa, baada ya kuropoka kwa niya ya kumtoka Mtui mbaya zaidi hakujuwa Mtui na Michael ni mtu na mjomba wake!



Ndani ya club hiyo, uliibuka mzozo uliozidi kumchanganya Michael Muganda kwani Marietha alimshika kiuno na kumvuta akitaka watoke nje, hakuelewa kwa kufanya hivyo ndiyo anamuharibia Michael ambaye alionekana kupigwa na bumbuazi la waziwazi,hakutambua ni kitu gani akifanye kwani Mjomba wake alikuwa tayari amekasirika anamuangalia kama chui.
“Honey tuondoke bwana,mimi nakuacha”
Marietha alimwambia Michael huku akimvuta kwa staili ya kumshika kiuno.Mtui alibaki akimuangalia Marietha, bado hakuwa tayari kuamini jambo analoliona ni uhalisia,alihisi kama hasira na kitu kama nyongo kipo ndani ya mdomo wake, hapohapo picha ya Deo akiwa gerezani ikampitia akilini na kumuona namna anavyoteseka.Hiyo ilimfanya apandwe na jazba zaidi na kumkata jicho kali la chuki Maerietha, aliyekuwa anamdekea Michael kimahaba!
“Anco…”
Michael alipata kitete sababu mbele yake alisimama Mjomba wake akiwa amevimba kama chura,hiyo ilimuogopesha kwani alijuwa huo ndio ungekuwa mwisho wake wa kusoma chuo.
Katika maswala ambayo yalimkera mjomba wake na alikuwa mkali kama pilipili ni linapokuja swala zima la elimu,hakuwa ana mchezo kabisa ndiyo maana hasira zake zilipanda mpaka kiwango cha juu kabisa akawa anahema juu juu pua zake zinamcheza, hiyo ilikuwa dalili tosha kuwa hakukuwa na usalama kabisa,uzuri wa Mtui siku zote hakuwa yupo tayari kuruhusu hasira zake zimtawale vinginevyo angechomoa bastola muda mrefu na Michael angekuwa marehemu siku hiyohiyo,alichofanya ni kugeuza na kuanza kutoka nje ambapo alienda na kusimama kandokando ya gari lake, kijasho jembamba kikiwa kinamtoka hiyo ni kutokana na hasira chafu alizokuwa nazo.
“Mtui Vipi?”
Sauti hiyo ilitokea nyuma yake kutoka kwa bwana Kakone aliyekuwa anakunywa naye bia.
“Acha tu Kakone”
“Upo sawa?”
“Ndio ndio,naomba tuhame hapa maana nitauwa mtu”
“Mtui mbona sikuelewi!”
“Kakone ingia ndani ya gari tuondoke,sitaki kwenda jela.Kama hutaki kuona ndugu yako nafungwa basi ingia ndani ya gari”
Wakati anaongea maneno hayo alimuona Michael anatokeza nje ya ‘Pub’ lakini hakutaka kuzungumza naye badala yake aliingia ndani ya gari,alivyohakikisha Kakone keshafunga mlango wa gari akageuza na kuondoka zake.
“Mtui,ilikuwaje pale?”
Bwana Kakone akaanzisha maongezi kwani alitaka kujua mkasa mzima!
“Bado sitaki kuaminiii”
“Kuamini nini?”
“Kuwa yule ni Marietha”
“Mariethaa,Marietha ganii??”
“Mke wa Deo…Embu subiri kidogo Kakone”
Niya ya Mtui ilikuwa ni kupotezea swali aliloulizwa na Kakone, ukweli ni kwamba hakuwa tayari kuongea lolote kwani aliamini kwa kufanya hivyo angemvua nguo rafiki yake Deo Karekezi,aliyekuwa anasota gerezani hivyo ilimlazimu akae kimnya na abaki nalo moyoni kwani hakuwa na sababu yoyote ya msingi ya kumwambia Kakone,hilo ndilo jambo alilolifanya na hasira zake zote na chuki zikahamia kwa Michael kwa kitendo alichokifanya.
“Mtui unaona vizuri lakini?”
Ni kitendo cha Mtui kuhama barabara na kuingia saiti nyingine, isingekuwa Kakone siku hiyo pembeni yake,wenda angepata ajali kubwa sana usiku huo na kuaga dunia hapohapo sababu mbele yake kulikuwa na lori kubwa la mizigo.Hiyo ni kutokana na hasira mbaya alizokuwa nazo na chuki,roho ilimuuma hasa alivyomkumbuka Deo Karekezi gerezani,akawaona siku ya harusi yao akiwa na Marietha wakiwa wenye furaha kifupi Deo hakustahili kufanyiwa unyama aliofanya Marietha.
“Shiiiiit”
Mtui alikema kwa hasira na kupiga usukani,jambo hilo likazidi kumchanganya sana Kakone akajuwa ni lazima rafiki yake hatokuwa sawa.
“Mtui una nini?”
“Kakone naomba nikuache kwako,tuonane kesho”
“Una uhakika utafika salama?”
“Ndio nitafika”
“Hapana,inabidi twende alafu mimi nitakodi bajaji au pikipiki”
Haikuwezekana hata kidogo kwa hali aliyokuwa nayo Mtui Kakone amtelekeze,alijuwa fika kuwa kuna tatizo linamsumbua lakini hakutaka kuhoji sana!Walivyofika Tegeta wakazidi kusonga mbele lakini huko kote Mtui hakuongea chochote zaidi ya kutiririkwa na majasho usoni.
“Nimefika”
Mtui akasema na kumgeukia Kakone baada ya kukanyaga breki nje ya nyumba yake,macho yake yalikuwa mekundu kama simba,usoni amekunja ndita, kulikuwa kuna kila dalili mbaya za hasira ndani ya kifua cha Mtui.
“Mtui una nini?”
“Niko sawa lakini nimefika”

**********
Michael aliogopa na alihofia, bado hakuamini kuwa aliyeonana naye alikuwa ni mjomba wake Mtui,alitamani swala hilo liwe ndoto ashtuke lakini haikuwa hivyo kwani ulikuwa ni ukweli mtupu na alichotakiwa kufanya ni kuomba msamaha haraka iwezekanavyo kwani Mtui ndiye alikuwa nguzo katika maisha yake,alihisi kujuta kwa jambo alilolifanya ndiyo maana alisimama nje peke yake akiwa anatembea tembea huku na kule akijaribu kutafakari ni jambo gani alifanye,Marietha nayeye hakuwa mbali alijaribu kumtuliza lakini haikuwezekana hata kidogo!
“Kwanini unawaza namna hiyo?”
Marietha ilibidi ahoji kwa mara nyingine,jinsi Michael alivyokuwa anazunguka zunguka huku kule ilimfanya ahoji.
“Marietha,unamfahamu vipi Yule mzee?”
Michael alitupa swali.
“Yule mzee?”
“Ndiyo,umemjuaje?”
“Ni stori ndefu baby lakini alikuwa ananitaka kipindi fulani hivi nilivyokuwa naishi Dar es salaam”
Kinywa cha Marietha kilinena uwongo,kitu alichokuwa anasema hakikuwa na ukweli wowote ule ndani yake na alijuwa fika kwamba anaongopa lakini aliamini kwa kufanya hivyo angelikingia kifua penzi lake.
Maneno hayo yalipenya moja kwa moja masikioni mwa Michael akayachukuwa na kuyapepeta, swala hilo lilikuwa gumu kwake kuliamini kwani alimuheshimu sana Mjomba na hata siku moja hakuwahi kuwaza kama angekuwa na mambo ya kihuni kama hayo.
Alibaki anamuangalia Marietha bila kum-maliza,alitamani kuongea kitu lakini alipata kigugumizi!
“Tuondoke”
Hilo ndilo neno aliloongea Michael akiwa hana furaha hata kidogo,walitafuta bajaji na safari ya kurudi hostel anayoishi kuanza.Hata walivyofika Michael hakuonesha aina yoyote ile ya uchangamfu, ilikuwa ni wazi kabisa mjomba wake alikuwa amechukia na mwisho wake wa masomo ndiyo ungekuwa siku hiyo, swala hilo lilikuwa nje-nje na hakukuwa na mjadala hata kidogo, ndiyo maana usiku kucha hakupata usingizi hata kidogo.
Hata Marietha alipojaribu kumtomasa ili amsisimue mwili na wafanye tendo lililowaleta duniani, haikufaa.
“Mariethaa,embu niache kidogo”
Michael alisema na kuutoa mkono wa Marietha uliokuwa kwenye mnara wake,ni wazi kuwa hakujisikia kufanya kitu chochote kile usiku huo.
“Unawaza nini?”
“Yule ni mjomba wangu unajua,ndiye anayejisomesha”
“Umeniambia”
“Wewe unadhani itakuwaje Marietha,hatoweza kunisomesha tena”
Michael alizungumza na kugeukia upande wa pili,moyo wake ulimuuma sababu alijuwa anaenda kukosa shule!

Asubuhi na mapema, siku iliyofuata alipokea simu kutoka kwa Mjomba wake Mtui, akimtaka aende nyumbani mara moja.
“Ndio..Anco sawa…ninakuja sasa hivi…Ndio ndio sasa hivi..Ndio,hapana.Naomba nisamehee..Sawa nakuja”
Ni sauti aliyosikia Marietha kutoka kwa Michael siku hiyo asubuhi lakini hakusikia upande wa pili nini kimezungumzwa ingawa alijuwa ni lazima atakuwa ni Mtui.
“Anco amenipigia simu”
Hatimaye akamwambia Marietha baada ya kukata simu na aliongea kwa upole hiyo ilimfanya Marietha anyong’onyee mwili mpaka akili.Ilikuwa ni wazi Kabisa kwamba Mtui atatoboa siri yake kuwa yeye ni mume wa mtu na Deo yupo gerezani hilo lilikuwa mbeleni kutokea.
“Ndiyo unaenda sasa hivi?”
Marietha aliuliza kitu kilichokuwa wazi kabisa!
“Ndio nataka niende sasa hivi”
“Sawa”
Marietha alikosa na alijuwa fika endapo Michael akirudi kutoka kwa mjomba wake ni lazima akili yake itakuwa imebadilika, hatokuja Michael Yule anayeondoka muda huo,ni wazi kuwa atapewa maneno ya ukweli ambayo yangemuumiza sana mtima wake.Marietha alijuta ni kwanini hakuongea ukweli siku zote,alijilaumu kwanini hakuzungumza na kuweka vitu wazi pengine angekuwa huru.
“Nimeamini ukweli humuweka mtu huru”
Marietha aliwaza huku akimshuhudia Michael akifungua mlango na kuondoka zake,baada ya hapo yeye alisimama na kuingia bafuni na kujiandaa,akachukuwa peni na karatasi kisha kuketi juu ya kitanda.
Ilionekana kuna kitu alikuwa anaandika juu ya karatasi na baada ya hapo aliweka juu ya kitanda,akachukuwa kila kilichokuwa chake kisha kufunga mlango na kuondoka zake!
*******
Hakuna siku aliyovimba kuliko siku zote kama hiyo,Mtui aliongea kwa jazba huku akitukana matusi mazito ambayo hayakuweza kuandikika kwa peni ama karatasi,mbele yake alisimama Michael, mtoto wa dada yake ambaye alimchukuwa na kumsomesha tangu utoto wake!Kushoto alikuwa ameketi Esta Muganda yupo kimnya machozi yanataka kumtoka,Michael alikuwa chini amepiga magoti anaomba msamaha, akijutia kitu alichokifanya.
“Nakuuliza wewe Mbwa,unamjua yule Mwanamke?Una mfahamu vizuriii?”
Mtui alizidi kufoka huku akitetemeka kwa hasira.
“Ndio Anco”
Jibu hilo lilijibiwa na Michael lakini alisukumwa na teke la kifua, likamdondosha chini chali.
“Kwanini umeniaibisha?Ni mara ngapi nimekuonya?Ni mara ngapi nakuuliza?Naongea nawewe kenge.Simamaa”
Mtui alifoka, hiyo ilifanya mpaka sauti yake ienee seble nzima,hata mkewe aliyekuwa pembeni aliogopa kwani hakuwahi kumuona mumewe akiwa katika hali kama hiyo!
“Yule mwanamke unamfahamu?Unajua nini maana ya kutembea na wake za watu?Unajua ana magonjwa gani?Mbona unataka kufa bado mdogo sana Michael”
“Naongea nawewe,unalia nini?Mimi napoteza pesa zangu kukusomesha wewe unaenda kutembea na wake za watu,tena mke wa rafiki yangu”
Kuanzia hapo Michael hakuzungumza chochote kile sababu alijuwa kwa kufanya hivyo angeshushiwa mguu wa shingo ingawa alitamani kuzungumza kwa niya ya kujitetea lakini hakutaka kujaribu kufungua mdomo wake.
Siku hiyo Mtui alizungumza kwa Machungu na moja kwa moja alimuhukumu Marietha kama Malaya mchafu,alijaribu kuunganisha matukio fulanifulani na kupata jibu la swali lake.
“Kumbe Deo alikuwa sahihi kabisa, nilikuwa nikimtetea Marietha,lazima ajuwe habari hizi.Hata kama atanichukia”
Mtui alimwambia mkewe kwa uchungu sana na alikuwa sahihi kufanya hivyo kwani ilimuuma jinsi Deo anavyoteseka gerezani, wakati huku nyuma Marietha mkewe wa ndoa anakula bata na maisha kwake yalikuwa ya raha mustarehee,afadhali angefanya hivyo mtu mwingine kuliko mkewe wa ndoa aliyekula naye kiapo kanisani kuwa mwili mmoja, hilo ndilo lililomuuma zaidi.
“Esta,kaka yako anatembea na mke wa mtu!Unalijua hilo?”
Swali hilo lilimuangukia Ester Muganda,dada yake na Michael.
“Hapana sijui”
Akazuga kwa kusema uwongo!
“Ndio nakwambia,hivi umemwambia kuwa kuna magonjwa mengi sasa hivi.Huyu mwanamke anayetembea naye ni mchafu.Alafu kuanzia leo utamsomesha wewe,mimi ndio mwisho, siwezi kusomesha mtoto malaya kama huyu……Nina imani sasa hivi una uwezo kufikia hapo mimi nimenawa mikono,msomeshe mdogo wako”
Macho ya Mtui yalikuwa mekundu hasira zake zilipanda mpaka juu kabisa na aliongea huku akitetemeka, hali hiyo ilikuwa mbaya sana.
Hakutaka kuendelea kubaki tena seblen alichofanya ni kuingia chumbani na kujifungia,mkewe alivyoona hivyo akaunga mkia mpaka chumbani ili kumpooza mumewe!
Mwisho wa masomo kwa Michael ilikuwa ni siku hiyo,hata yeye aliumia sana moyoni, kupewa historia nzima ya Marietha na kisa cha mumewe kuwa gerezani.Alimchukia sana Marietha kumdanganya na hakuelewa angefanya nini kama ikitokea akimkuta geto kwake.
Michael aliondoka taratibu!
“Sasa unaenda wapi?”
Ester alimuuliza kaka yake!
“Naenda hostel”
“Michael,Make sure unamuomba msamahaa Anco.Leo ana hasira njoo kesho asubuhi,mimi nitajitahidi kuongea naye,ikishindikana nitajuwa cha kufanya”
“Sawa sista mimi naenda”
Hapohapo Michael aliondoka,alichukuwa daladala mpaka Ubungo ‘Riverside’ ambapo alikodi pikipiki ili afike anapoishi,hasira zake ilikuwa ni azibwage kwa Marietha na alitamani afike wakati huohuo!Kitendo cha kushuka na kumlipa dereva ujira wake,alitembea mpaka sehemu aliyopanga,bila kugonga hodi alinyonga kitasa na kuzama ndani.
“Mariethaa,Mariethaa”
Aliita na kuingia bafuni lakini Olaaa!Marietha hakuwepo,alivyopiga jicho kitandani akaona karatasi nyeupe,akaikwapua na kuigeuza.
*******
Habari alizopewa Marietha baada ya kufika Mkoani Tanga,nyumbani kwake,zilimfanya aporomoke mpaka chini na kuanza kulia kwa sauti ya juu sana ni dhahiri kwamba alikuwa ameingia kwenye matatizo mengine baada ya kuyachenga kwa kipindi kirefu kidogo!
“Rebe..ca ongea ukwe..li Abraha..m amefanya nini?”
Marietha aliuliza tena bado hakutaka kukubaliana na habari alizopata kutoka kwa Rebeca, jirani ambaye kabla hajaondoka alimuachia watoto wake.
“Ukweli ndi..o huo Marietha”
“Kwani..ni sasa hukunipigia simu?”



Moyo wake ulimuuma kama Mama alihisi uchungu ajabu,hata hivyo alijuta na kuapia kwamba hatorudia tena kosa, alidiriki hata kujiita Mama mjinga na mpumbavu kwa kitendo alichokifanya na kuapa kubadilika,watoto wake walikuwa kila kitu kwa wakati huo.Habari za Abraham kuvunjika mguu ndizo zilimfanya achanganyikiwe zaidi na zaidi!
Kwake lilikuwa ni pigo kubwa sana sababu alimpenda mwanaye kuliko kitu chochote kile chini ya jua la Mungu ingawa alikuwa akimuacha mwenyewe na kwenda kufanya starehe hiyo haikumaanisha kwamba hampendi au hawapendi watoto wake,La hasha ni starehe tu za muda mfupi zilikuwa zinamzuzua.
“Yuko wapi Abr..aham sasa?”
Aliuliza kwa kwikwi huku bado akiwa chini.
“Yuko hospitali”
“Na William yuko wapi?”
“Yeye amelala”
“Kuna mtu wa kumwangalia?”
“Ndio”
“Basi nipeleke Hospitali nikamuone Abraham”
“Sawa,twende”
Njia nzima Marietha alikuwa akimwaga machozi ya uchungu na alihisi kujuta kwa mambo aliyokua anafanya, wakati mwingine alidhani wenda ni pepo ndilo lilimpelekea mpaka akawa zuzu na teja wa mapenzi,pepo huyo akamfanya mpaka awasahau watoto wake aliyowavaa kwa uchungu.
“Mimi ni Mama gani,nisiyekuwa na uchungu na watoto wangu?”
Marietha alitafakari wakiwa njiani na Rebeca wanatembea kuelekea katika hospitali ya wilaya ambayo iliyokuwa jirani tu hapo,ulikuwa ni mwendo wa kama mita mia moja na mbili hivi mpaka hospitali hiyo ndogo aliyolazwa Abraham.Walivyofika tu moja kwa moja walionana na Dokta na kutoa maelezo.
“Mtoto anaendelea vizuri.Tumemfunga POP mguuni,baada ya wiki moja utamleta ili tuone maendeleo yake”
Nyuma ya meza hiyo alizungumza mwanaume mwembamba kidogo,kijanakijana lakini machoni alikuwa amevaa miwani, koti kubwa jeupe huyu alikuwa bingwa wa kutibu mifupa ya binadamu aliyefahamika kwa jina la dokta Peter Misango.
“Sawa Dokta tumekuelewa,kwahiyo tunaweza kwenda naye?”
“Ndiyo lakini tu muwe makini naye”
“Sawa ni kiasi gani?”
“Labda muende pale nje kwa basa atawapa bili yenu”
“Ahsante”
Aliyekuwa anazungumza na Daktari alikuwa ni Rebeca,Marietha hakuongea chochote sababu alijisikia kulia na alijiona yeye ni mkosaji, vitu vingi sana vilipita kichwani kwake akaenda mbali kifikra.
Walivyosimama kutoka ofisini kwa daktari wakapitiliza moja kwa moja nje kaunta ambapo walifanya malipo yote na kununua dawa za kutuliza maumivu,wakaonyeshwa wodi alilolazwa Abraham,baada ya Marietha kumtia mwanaye machoni alishindwa kuzuia machozi yake,hapohapo alianza kulia.Mguu wa Abraham mmoja ulikuwa umening’inizwa juu.Lakini alikuwa amelala na aliamini mwanaye yupo katika mateso makali ya maumivu.Mtoto Abraham alikuwa kama amehisi kwani alifungua macho yake na kuona sura ya Mama yake,furaha aliyokuwa nayo ilimfanya mpaka asahau kama ana mguu mbovu, akamsogelea kwa shida Mama yake na kumkumbatia kwa nguvu zote ingawa mguu wake mmoja ulikuwa upo juu,wote wakawa wamekumbatiana kitandani!
“Mama usiniache tena”
Abraham alisema, hiyo ilimfanya Marietha azidi kumwaga machozi kwani alijihisi uchungu kupita kiasi.Abraham aliruhusiwa hospitali,maisha yakaendelea kama kawaida na Marietha aliapa kujirekebisha,alitokea kuwapenda sana watoto wake na aliapa hatowaacha tena na mara kadhaa alikuwa akisema kuwa shetani alitaka kumtumbukiza ndani ya shimo refu ambalo hata angeshushiwa ngazi asingeweza kupanda.
“Acha nianze maisha mapya”
Marietha alijisemea siku hiyo akiwa nje anafua nguo zake huku Mtoto William akiwa pembeni yake anacheza,William alimkumbusha mbali sana alimrudisha kifikra siku ya kwanza anaenda na mumewe Deo Karekezi nchini Ufaransa kisha akabakwa ndipo akatokea William, mtoto huyo akaleta vita kubwa ndani ya ndoa yake,hata hivyo aliyatupilia mbali mawazo hayo na hakutaka kukumbuka tena habari zilizopita nyuma.
“Mamaaaaa Mamaaaaa”
Abraham aliita akiwa ndani.
“Abraham unasemaje mwanangu?”
“Maji ya kunywa”
“Nakuja”
Umri aliokuwa amefikia Abraham ulitosha kabisa kunasa maneno na kutambua vitu na mbali na hapo alikuwa mtoto msikivu na mwelevu,hilo lilikuwa gumzo pia.
Sio siri mtoto huyu alikuwa ana kila sifa ya kuitwa Malaika, alikuwa ni mzuri kadri siku zilivyozidi kwenda mbele,kutokana na Marietha kuamua kubadilika ilibidi macho yake yote yawe kwa watoto wake,wakanawiri na wakazidi kupendeza zaidi na zaidi.

Likizo ya kazi ilivyoisha, Marietha alirudi kazini na kuendelea na kazi kama kawaida kwani Abraham mguu wake ulikuwa una afadhali,hakutaka tena kujiingiza kwenye maswala ya mapenzi,alitaka kulea wanaye na kuwatunza vizuri.
Marietha aliendelea kufanya kazi kwa bidii zote na kujituma,mwaka mmoja ulivyopita ilibidi awaanzishe watoto wake ‘Baby class’ ili wakajichanganye na watoto wenzao na kuhusu swala la ada lilikuwa juu yake.Kitendo cha Abraham na William kuanzishwa shule hiyo iliyoitwa Edeyan Baby class liliibuka gumzo la ajabu kwani kila mwalimu aliwashangaa watoto hao kwa namna walivyokuwa wazuri.
“Hiki kitoto cha Kike au cha kiume?”
Siku hiyo Madam Magreth alishindwa kukaa na dukuduku moyoni mwake, ilibidi amuulize mwenzake.
“Si unaona kavaa kaptula,cha kiume hicho kitoto!Mdogo wake sasa umemuonaaa?”
“Mdogo wake huyo mtoto?”
“Ndio,kama mzungu fulani hivi.Huyo baba yao atakuwa ana mbegu nzuri sana!Angekuwa jogoo au Mbuzi ningemnunua”
Walimu siku hiyo badala ya kufundisha walikuwa wakiwajadili Abraham na William,walikuwa ndani ya ofisi zao wanakunywa chai huku wakiwaangalia Abraham na William wanavyocheza.
*****
Saa,dakika,Sekunde zilikatika!Majuma yakapita,miezi ikasogea,hatimaye mwaka mwingine ukaisha kama utani.Hiyo ilikuwa changamoto kubwa kwa Marietha kwani yeye ndiye alikuwa baba na Mama pia,alilivaa jukumu la kuwalea watoto wake na aliwapenda kutoka moyoni.
“Mama,leo wanafunzi wote walikuja na baba zao.Baba yetu yuko wapi?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Abraham siku hiyo lilimshangaza sana Marietha bila kutegemea,alikuwa anapika jikoni akaganda na kugeuka.
“Abraham,nikupe chakula?”
“Hapana nimeshiba,kwani baba yetu yuko wapi?”
“Baba yenu yupo lakini amesafiri”
“Atarudi lini?Mpigie simu”
“Nitampigia”
Marietha alitamani kuongea ukweli lakini alishindwa mbali na hapo moyo ulimuuma,mawazo yake yakasafiri kwa kasi sana yakampeleka siku ambayo alijifungua Abraham,akamuona mumewe Deo alivyokuwa mwenye furaha,akamzawadia na gari ya kutembelea.Vitu vingi sana vilimiminika ndani ya akili yake akawa kama anaangalia sinema ya kihindi mbali na matatizo mbalimbali na tofauti tofauti kumuandama lakini siku zote alijuwa kuwa Deo ndiye kila kitu katika maisha yake,alitamani aende gerezani na kumuona lakini alishindwa sababu aliona aibu kwani alijua ni lazima Mtui amepeleka taarifa zake kuhusu yeye na Michael Muganda!
Jambo ambalo lililomfanya anyong’onyee na kumlazimu ajutie kwa kitendo alichokifanya.
Licha ya kuwaza sana hakutaka kuendelea kujipa ‘stress’!Hakutaka kukumbukua tena ya nyuma kifupi alishafungua ukurasa mpya wa maisha yake.
Mbali na kuwaambia wanaume wanaomtongoza kuwa ana watoto lakini walimgasi na kumsumbua sababu uzuri wake ulikuwa palepale na ulizidi, ungemwangalia kwa harakaharaka ungedhani wenda ni binti mdogo wa miaka ishirini na mbili,sio siri Marietha bado aliendelea kuwanyanyasa wazee kwa vijana!
“Hata kama una watoto.Hata mimi nina watoto pia”
“Sasa mimi unanihitaji wa nini?Baki na watoto wako namimi nibaki na wangu”
“Acha nikusaidie kulea watoto hao”
“Usijali mzee wangu,nitawalea mwenyewe,hawana shida yoyote ile”
“Huwezi,lazima upate kidogo mwanaume wa kukaa naye.Mtu kama mimi,nina pesa eeeh,Nina nyumba.Ukinikubalia nitakujengea nyumba au nitakupa nyumba moja au chagua”
“Nashukuru Mzee”
Hiyo ilikuwa mistari ya Mzee Manjama akijaribu kutupa jiwe gizani, akimuimbisha lakini jitihada zake ziligonga mwamba kwani alikataliwa na Marietha alimchomolea,kifupi alishabadili mienendo ya maisha yake!Kutongozwa kila siku na wanaume tofauti tofauti ilikuwa ni sehemu ya maisha yake hiyo ilitokana na uzuri aliokuwa nao,kwa umri aliokuwa nao hakuwa na haja tena ya kujiingiza kwenye mapenzi sababu hakukuwa na kitu kingine kipya zaidi ya mateso, hivyo aliamua kugeuzia maisha yake kwa watoto wake wawili Abraham na William,sio siri aliwapenda sana na alikuwa yupo tayari kupambana na mtu yoyote yule atakayetaka kuwachukua kutoka mikononi mwake.
Ratiba ya Abraham pamoja na mdogo wake Wiliam ama pacha wake kama walivyozoea kuwaita shuleni ilijulikana kwamba saa mbili asubuhi wanaenda shuleni na saa kumi jioni wanatoka,kutokana na majukumu ya kikazi ilimuwia vigumu kwa Marietha kuwachukuwa watoto wake kutoka shule, hivyo alimuajiri jamaa mmoja jirani yake ambaye hata yeye alikuwa ana watoto wake wadogo wanaosoma na Abraham pamoja na William,kwa wiki alikuwa anamlipa shilingi elfu tano.
“Mama watu wanitania shuleni mimi mzuri,wanasema nafanana na msichana”
Siku hiyo Abraham alilalamika, ilielekea swala hilo lilimfika shingoni.
“Achana nao mwanangu,kwani wewe unapenda kuwa mbaya?Mbaya ni shetani,mtu akikwambia wewe mzuri sema ahsante!Sawa?”
“Sawa Mama,alafu leo mimi na William tuliitwa kwa Madam ofisini kwake akatupa chai na chapati,kasema anatupenda sana siku moja atatupeleka kwake”
Ulikuwa ni uwazi mtupu,walimu walivutiwa na watoto hao wawili waliotisha kwa uzuri wa kipekee,katika historia ya shule hiyo haikuwahi kutokea, hata wazazi wa watoto wengine walivyowaona Abraham na Wiliam walivutiwa nao,sio siri watoto hawa walikuwa homa ya jiji!
Kama ilivyokuwa kwa wazazi waliowaona Wiliam na Abraham na kuwatolea udenda ndivyo ilivyokuwa kwa wanaume waliomuona Marietha,kila mtu alitumia pesa zake kumnasa lakini hakutingishika hata kidogo kwani alishaupiga moyo wake ‘stop’ kupenda tena na kujiingiza katika swala zima la mapenzi.
“Sawa hata kama wewe ni Tycoon wa hili jiji,ni wewe.Pesa ni zako sio zangu”
“Ukinikataa mimi ni sawa na kutupa gunia la pesa chooni,ngoja nikwambie ukweli.Leo umekutana na pesa ana kwa ana”
“Basi mimi nina mume tayari.Na ananitosha pesa sio kitu,mapenzi hayatengenezwi benki Mzee wangu, bali yanatengenezwa moyoni”
Marietha akaibuka na hoja ya kumchomolea Mzee huyu tajiri aliyefahamika kwa jina la Mtumbuka Maximo,alikuwa ni muwekezaji mkubwa ndani ya mkoa huo wa Tanga na jina lake lilikuwa katika chati ya matajiri waliokuwa wanatingisha jiji hilo la Tanga,kifupi Marietha hakujua kuwa anaongea na Milionea.
Kutokana na pesa alizokuwa nazo Mr.Mtumbuka Maximo aliamini kumpata Marietha ilikuwa ni sawa na kuweka kikombe cha juisi mdomoni,lakini kwa bahati mbaya ilikuwa kwake kwani Marietha alimkatalia na kusimamia msimamo wake.
“Baruti fuatilia huyu mama anaishi wapi”
Alivyoingia ndani ya gari alitoa ujumbe huo kwa mmoja wa walinzi wake.
“Sawa bosi”
Magari sita ya kifahari yakaondoka eneo hilo wakati huohuo.Baada ya dakika moja kutoka tu,wafanyakazi wa hoteli hiyo walimfuata Marietha na kuanza kumuhoji maswali kwani walimfahamu tajiri huyu hatari mwenye pesa za kutishia amani ya mkoa!
“Yule mzee unamfahamu Marietha?”
Mmoja wa mashoga zake alihoji,alitaka kujuwa ilikuwaje akakaa na Marietha kwa muda mrefu.
“Wazee hawa wasumbufu sana,sina haja ya kumfahamu”
“Weeeeee,acha masihara.Huyu mzee ndiye milionea hapa Tanga nzima huyu mzee ni Don,ni tajiri.Ni tycoon Yule ana maweee.Unamfahamu au unatuigizia?”
“Mimi simjui,amekuja hapa nimemuhudumia vizuri nashangaa kaniita nikae,nikamwambia nipo kazini. Kwanza alikuja jana hapa pia….”
“Una namba zake?”
“Za nini?”
“Za niniiiiiii?!Hivi Wewe Marietha una wazimu?Unakisikia unachokisema?Ngoja nikwambie vizuri shoga ili unielewe Yule mzee anakimbizana na akina Manji kwa pesa,hakuna asiyemjua hapa”
“Sasa unataka kuniambia nini?”
“Changamkia tenda hiyo,ohoooo.Ndio njia yako pekee ya kuuaga umaskini”
Wafanyakazi ama mashoga zake walimshawishi Marietha alegeze uzi kwani alikuwa anacheza na shilingi kwenye tundu la choo!
*****
“Kaniiitie meneja wenu aje hapa”
Ilikuwa ni sauti kutoka kwa mzee huyu tajiri akiwa amefika nje ya hoteli aliyokuwa anafanyia kazi Marietha na niya yake ilikuwa aonane na meneja wa hoteli.Hapohapo, aliitwa na kuambiwa akae kwenye kiti.
“Habari yako kijana”
Mzee alianza kutoa salamu baada ya meneja kukubali wito.
“Nzuri mzee shikamoo”
“Marahaba,hapa una wafanyakazi wangapi?”
“Wahudumu?”
“Ninaposema wafanyakazi nina maanisha mpaka wafagiaji wa chooni”
“Wafanyakazi Thelathini na nane”
“Well,Kwa siku huwa una uza kiasi gani cha pesa?”
“Milioni tano mpaka sita”
Meneja wa hoteli hiyo alimfahamu sana mtu aliyekuwa mbele yake na ndiyo maana alijibu maswali kiufasaha na adabu zote!
“Nina taka kufanya mazungumzo,sitaki kuona hata mtu mmoja.Kifupi ni kwamba nitakupa milioni sita sasa hivi,utoe wateja wote humu ndani.Na wafanyakazi uwaambie wakapumzike”
Mzee huyu pesa hizo zilikuwa niza kununulia maji tu,ndiyo maana hakuona hasara yoyote ile na niya na madhumuni yake alitaka kuongea na Marietha amwambie ni jinsi gani ametokea kumpenda na alijisikia kumuoa pia.
Hivyo ndivyo moyo wake ulimsukuma afanye jambo hilo! Hakukuwa na muda wa kupoteza, wateja waliofika siku hiyo waliinuliwa na kuambiwa kuwa kuna dharura ya ghafla imetokea na kila mtu alilipwa pesa yake.
“Marietha Usiondoke”
Bosi ama meneja alimzuia Marietha asitoke kazini kwani Tycoon Mtumbukka Maximo alihitaji kuzungumza naye!



Pesa na mali alizokuwa nazo Mzee Mtumbuka Maximo zilitishia amani sababu hata yeye alijuwa,kwa uwezo aliokuwa nao aliamini kumpata Marietha lilikuwa jambo rahisi sana kwake sababu aliamini kuwa pesa ni sabuni ya roho na hakuna mwanamke yoyote ambaye akiingiliwa kwa gia ya pesa, angechomoka licha ya yote hakumtamani Marietha bali alimpenda kweli kutoka moyoni,ndiyo maana aliacha shughuli zake zote na kumpigia mingo,mitego na mikakati aliyopanga kuifanya ilikuwa ni lazima Marietha ajae kwenye kumi na nane zake.
Siku hiyo alivyotoka nyumbani kwake akiwa na jopo la walinzi pamoja na msafara wa magari saba alipanga kwenda kukutana na Marietha katika hoteli aliyomkuta.Na ndicho hiko kilichotokea, baada ya kukodi hoteli akitaka wateja wote waondoke mara moja,meneja alivyoitwa aliandikiwa hundi ya milioni sita hapohapo,hazikupita dakika mbili Marietha akawa amefika mbele yake lakini sura yake ilikuwa imejikunja kiasi,alionekana kukerwa sana na gasia za Mzee huyo aliyekuwa anamtongoza kila wakati.
“Lakini mbona unanisumbua hivyo?Si nimekwambia usinifuate fuate,nipo kazini”
Marietha alionesha kufoka kwa jazba.
“Naomba mtupishe kidogo”
Mzee Maximo aliwaambia walinzi wake waliokuwa pembeni wamevalia suti nyeusi,kooni wamenyonga tai, sio siri mzee huyu alilindwa kama rais wa nchi,walinzi wote wakatoka kando kama mita tano hivi ili kupisha faragha ya bosi wao lakini macho yao yalikuwa hapohapo wakiangalia usalama wa tajiri yao.
“Kaa chini Marietha,usijali kuhusu kazi yako.Nishaongea na bosi wako”
“Hata kama”
“Nakuomba ukae”
“Siwezi,nikae kufanya nini?”
“Kaa tuongee mawili matatu.Unajuwa nataka kukuambia nini?”
“Sitaki kujua”
“Nakuomba ukae,nipe dakika mbili tu za kunisikiliza kisha nitakuruhusu nakuomba tafadhali”
“Dakika moja tu nakupa”
“Okay”
Marietha akavuta kiti na kukaa,kwa sharti la kwamba angempa muda wa dakika moja Mzee Maximo.
Hapo ndipo mzee huyu alipoanza kuelezea kuhusu mipango yake na alimuambia kila kitu kuhusu yeye na maisha yake na utajiri wake kwa ujumla,alimueleza ni kiasi gani angeyabadili maisha yake na angeishi kama malkia.Hilo lilikuwa wazi kabisa kama Marietha angekubali kwani Mzee Maximo alikuwa mwenye niya hiyo,uzuri wa Marietha ulimuingia moyoni na akahisi kumchukuwa mazima kwa gharama yoyote ile.
“Nina mke na watoto kama nilivyokwambia Marietha lakini nakuhakikishia kuwa hapa duniani utaishi kama malkia,hautosumbuliwa na mtu yoyote yule”
“Kwanini usitulie na mkeo sasa?”
“Nimekupenda wewe hapo,pia ninaipenda familia yangu vilevile.Lakini mimi nakupenda zaidi”
“Mkeo akijua je?”
“Hilo niachie mimi”
“Hapana siwezi,tafuta mwanamke mwingine”
Marietha mara ghafla akaanza kuwa vuguvugu sio baridi,sio moto!
Hilo halikumuumiza sana Mzee Maximo na kuanzia siku hiyo hakukauka hotelini hapo,aliapia atafanya juu chini swala lake lizae matunda,alizidi kumuwinda Marietha kila kukicha akitumia mbinu tofauti tofauti za pesa.
Kitu kilimchofurahisha zaidi ni baada ya kuambiwa ni wapi Marietha anaishi yaani kwa wazazi wake.Wiki moja baadaye alimwambia dereva wake waongozane mpaka Maduda.
Ilikuwa ni safari ndefu kiasi ndiyo maana walitumia gari aina ya Marcedez benz na gari zake zote kwenye namba za Usajili zilikuwa na jina lake ‘Mtumbuka Maximo’ sababu hiyo tu ilifanya iwe rahisi kugundulika kuwa anapita eneo hilo na akipita sehemu yoyote ilikuwa ni lazima watu wakigeuza shingo zao kuangalia msafara wa magari unavyoenda,sio siri mzee huyu alikuwa ana pesa nyingi sana kiasi kwamba hata punda angebebeshwa asingepiga hatua!
Msafara wa magari ya Maximo ulianza saa tano ya asubuhi ukisindikizwa na magari mengine saba,gari la katikati ndiyo alikuwa yupo yeye pamoja na mlinzi wake mmoja kiti cha mbele!Kutokana na utajiri wake huo wa ajabu serikali iliamua kumfuatilia wakidhani wenda anajihusisha na biashara haramu za madawa ya kulevya,walimgasi lakini aliwaonesha nyaraka zote za ulipaji kodi TRA na jinsi utajiri wake alivyouvuna,hapo walimuachia lakini aliisumbua serikali bado.
Masaa matatu baadaye, wakawa wamefika shule ya Maduda wakakunja kushoto kama walivyoelekezwa kuwa Marietha ndipo alipokulia.Msafara ukasimama nje ya nyumba iliyojengwa na matofali lakini imechoka na nje haikuwa na rangi.Walinzi wakaanza kushuka kuangalia usalama wakakagua kama dakika moja nzima ndipo mlango wa Maximo ukafunguliwa,akatanguliza kiatu cheusi na kushuka.Tukio hilo lilifanya nyumba za jirani wajifungie ndani na kubaki kuchungulia madirishani.
“Nadhani ni nyumba hiyo hapo”
Maximo aliongea huku akionesha nyumba ya akina Marietha,alikuwa ana uhakika na anachokisema kwani mitaa hiyo aliijua na nyumba hiyo alikuwa ana uhakika ndiyo yenyewe kwa mujibu wa meneja wa hoteli aliyekuwa anafanyia kazi Marietha.
“Ngo! Ngoo! Ngooo!”
Mlio wa Mlango ndio uliosikika ukigongwa! Dakika mbili baadaye likasikika komeo linafunguliwa kwa ndani!Sura zilizokuwepo nje zilimshangaza Mama Samson,wingi wa magari nje ulimshtua zaidi.
“Samahani kwa ugeni wa ghafla lakini naomba nikaribishe ndani,ninahitaji kuzungumza nawewe.Mimi naitwa Maximo,ni rafiki yake na Marietha”
Siku zote mzee huyu alikuwa ni mstaarabu sana ndiyo maana alianza utambulisho ili kumtoa wasiwasi mama huyu aliyeonekana bado kuduwaa,Maximo alikaribishwa ndani akaingia na walinzi wawili huku wengine wakizunguka nyumba na kuiweka katikati ili kulinda usalama wa tajiri yao!Maximo hakutaka kuzunguka mbuyu moja kwa moja akasema jambo lililompeleka nyumbani hapo na katika maongezi yake alilitaja jina la Marietha na kusema ni kiasi gani anampenda kutoka moyoni na alikuwa yupo tayari kufanya lolote lile juu yake.
“Mimi ni mama yake mkubwa,Mama yake alifariki.Kwahiyo nimekuwa kama Mama yake sasa.Sawa tunakubali lakini mimi kama mimi siwezi kuusemea moyo wake,ongea naye mwenyewe sababu keshakuwa mtu mzima”
Mama Samson nayeye alitoa hoja yake na kuhitimisha.Mzee Maximo na Mama Samson siku hiyo walimjadili Marietha kwa masaa mengi sana na baadaye mzee huyu alivyoondoka alichomoa bunda la shilingi milioni mbili, akamkabidhi Mama Samson!
“Utanunua matunda ule Mama”
Macho yalimtoka Mama Samson, hakuamini kama milioni mbili zilikuwa zake na anaambiwa akanunue matunda,jambo lililomfanya amuone kama Maximo ni Mungu wake wa pili mbali na hapo kipindi hicho pesa zilikuwa hakuna!
“Ahsante Baba lakini zungumza na Marietha,mimi nitamuita niongee naye”
“Alafu kitu kimoja,hii nyumba nitaikarabati”
“Hii nyumba?”
“Ndio,nitaikarabati.Itakuwa ya kisasa.Sitaki mwanamke ninayempenda aishi kama hivi”
Maximo hakuwa mzee mwenye longolongo na katika sentensi yake hakukuwa na tone la mzaha hata kidogo kwani mwezi mmoja baadaye wakandarasi walifika na kuanza kuikarabati nyumba nzima,wakati mafundi wanafanya ujenzi yeye kazi yake ilikuwa ni kumuimbisha Marietha akubali ombi lake na swala hilo Mama Samson aliliingilia katikati akamshinikiza amkubali tajiri Maximo.
“Lakini Mama,si unajua mimi ni mke wa mtu”
“Mke wa mtu?Mke wa mtu Bongo,Deo hana kitu sasa hivi.Wewe unafikiri atakupa nini sasa hivi yupo huko gerezani.Hivi wewe ukae miaka Kumi na tano,Marietha unachekesha wewe,yaani sijui umekuwaje.Embu rudia tena”
“Mimi ni mke wa mtu.Deo ni mume wangu”
“Maximo anajua?”
“Hapana hajui”
“Basi usimwambie”
“No,Mama lazima ajuwe ukweli wote,ili ajuwe cha kuamua”
“Angalia tu usimpoteze huyu mzee”
“Kwani lazima kuwa naye?”
“Embu tazama hii nyumba anavyotujengea.Utampata wapi mwanaume wa namna hii usawa huu”
“Kwahiyo mama hilo ndilo limekupagawisha”
“Sio hilo tu.Utakuwa na heshima kubwa,huyu mzee unamfahamu sawasawa?”
“Heshima?Au nitajidhalilisha,mke wa mtu”
“Marietha bado mdogo mwanangu ndio maana huelewi,lakini ipo siku utajuwa nini nina maanisha”
Mama Samson alitumia ushawishi mkubwa sana na pesa alizokuwa anapewa na Mzee Maximo zilimzuzua,kazi yake ikawa kama kuwadi na aliamini jambo hilo lingefanikiwa kwa muda mchache na angeendelea kuvuna pesa za Mzee Maximo kiulaini.

*********
“Lakini mimi nina Mume na nina watoto wawili.Ndiyo maana inakuwa vigumu,huo ndio ukweli wangu Maximo samahani kwa kukuficha kwa muda mrefu,mimi huwa sipendi mambo yangu yawe wazi kila mtu ajuwe”
Siku hiyo Marietha aliamua kufunguka,aliamini kwa kuongea hayo atakuwa huru na hata kama Maximo akiendelea kumpenda hivyohivyo hilo lisingekuwa kosa lake tena.Maximo,alibaki akimtizama Marietha machoni bila kummaliza ilielekea habari hizo zilimshtua na zilikuwa ngeni kwake!
“Ukipenda ua penda na boga lake.Mumeo yuko wapi kwani?Anaishi wapi?”
“Hayupo,yupo gerezani”
“Pole sana,alifanya nini?”
“Tuachane na hayo”
Kwa Marietha kuwa na watoto pamoja na Mume hilo halikumtingisha Maximo,akazidi kumshawishi Marietha na mwisho wa siku Marietha alishindwa kushikilia msimamo wake kwani kila aliyemfata kumuomba ushauri alimwambia kuwa atajutia sana endapo akimchomolea Mzee huyo tajiri Maximo,hapo ndipo alipojikuta ameingia kwenye penzi la Maximo na baada ya mwaka mmoja Maisha ya Marietha yalibadilika sana,alinunuliwa nyumba kali ya gorofa tatu pamoja na gari la kifahari la kutembelea,kufumba na kufumbua akawa anaishi na watoto wake, maisha ya kishua na angejisikia kujuta endapo angemkataa Maximo.
********
Deo Karekezi aliendelea kusota gerezani na siku zote hakuacha kukumbuka maisha yake ya uraiani, jinsi alivyokuwa mfanyabiashara mkubwa na mwenye mali,kichwa chake kilizongwa na vitu chungu mzima hususani alivyomkumbuka mke wake wa ndoa Marietha,aliapia endapo akitoka gerezani angemfuata na kuanza tena kujenga maisha yao upya ingawa aliamini kuwa angeanza moja,kifupi kufumba na kufumbua angerudi uraiani akiwa kapuku yaani oheahe maskini wa kutupwa,miaka kumi na tano bado ilikuwa mingi kwake na masaa yalikuwa yanajisogeza kwa mwendo wa kinyonga!
Kitu kilichokuwa kinamuumiza kichwa chake siku zote ni Marietha,zaidi ya mwaka mmoja na nusu ulipita hakumtia machoni na kila alipokuwa anajaribu kumuuliza Mtui hakupewa jibu lililonyooka.Wakati mwingine alihisi wenda kuna kitu kibaya kinaendelea ama Marietha alikufa siku nyingi lakini wanamficha,mawazo mengi mabaya yalikizonga kichwa chake lakini aliyatupilia mbali mawazo hayo na kuyaita mawazo hayo yakishetani kwani hakutaka kumfikiria mke wake vibaya tena!
“Mtui niambie ukweli leo, Marietha yuko wapi.Mbona unanipiga chenga kila nikikuuliza hilo swali”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Deo,akimuuliza Mtui siku hiyo ya kuwaona wafungwa ilipofika.Mtui alikuwa ana siri kubwa sana kifuani kwake ambayo aliamini angeitoboa ingemuumiza sana Deo mtima, kwa maana hiyo hakutaka kufungua mdomo wake ingawa moyo wake ulikuwa na shauku kubwa wa kulisema jambo hilo.
“Marietha yupo lakini sijamuona siku nyingi hata mimi.Mara ya mwisho aliniambia anakupenda sana”
“Alisema ananipenda?Mwambie nimemmisi.Awe anakuja basi,amenenepa?”
“Anaendelea vizuri lakini mawazo tu ya hapa na pale”
“Msalimie sana,aniandikie basi hata barua”
“Nitamwambia”
“Watoto wangu hawajambo?”
“Wote wazima.Wangekuwa wanaumwa Marietha angenieleza”
Vitu alivyokuwa anazungumza Mtui kumwambia Deo vilikuwa ni tofauti kabisa,kwani Marietha alishabadilika na alimfuma na Michael Muganda,isingekuwa busara alizokuwa nazo basi angeropoka kila kitu.Kipindi kigumu alichokuwa nacho Deo haikuwa sahihi kabisa kumwambia mambo kama hayo ambayo yangemfanya ajisikie uchungu zaidi na zaidi.
Katikati ya maongezi yao walishtuliwa na Msichana mwenye umbo dogo na sura hiyo ilikuwa ngeni kwa Mtui lakini Deo alimkumbuka vizuri sana,ndiyo maana alishtuka na kubaki anamtumbulia macho!
“Leilaaaaa”
“Deoooo.Oooh God have Mercy!”
Alikuwa ni Leila!Watu hawa wawili walikuwa na historia nzito sana huko nyuma na hakuna hata mmoja kati yao aliyekuwa tayari kuamini kamuona Mwenzake,Leila alishtuka zaidi baada ya kumuona Deo yupo ndani ya sare za magereza.
“What happened Deo?Sielewi,make me understand!Why are you here?”
Leila alizidi kushangaa na kukoroga kizungu kama kawaida yake,alimuangalia Deo kwa masikitiko makubwa sana na moyo wake uliingiwa na huruma.
“First of all I’m so sorry Deo.Let’s keep our differences aside.I know we had bad history.Lakini naomba nikwambie kitu kimoja,maisha yangu niliamua kuyaweka kwa Yesu Kristo wa Nazareth aliyemwaga damu pale msalabani kwa ajili ya dhambi zetu”
Deo bado alikuwa ameganda,anamtizama Leila anayesema kuwa amebadilika, bado hakutaka kuamini kama yupo mbele yake kwani hata siku moja hakudhani kuwa angekutana na kiumbe kama huyu katika maisha yake,katika kumsikiliza kwake akamuomba akae chini ili waongee na kumwambia mkasa wote uliotokea,kinagaubaga!
“Ndio hivyo Leila,mimi nimekusamehe.Huyu anaitwa Mtui.Ni zaidi ya ndugu yangu”
“Deo,trust me.Utatoka,nitakuweka kwenye maombi na nitapambana,nina maanisha kusema haya believe me or not”
Deo hakuyatilia maneno ya Leila maanani kwani alizoea tu alikuwa muongeaji na lopolopo,hakujuwa kuwa ilikuwa tofauti kabisa sababu Leila alikuwa ana maanisha kwa kile anachokiongea.
“Naenda kukata rufaa Deo,I will start from there”
Baada ya hapo walipiga stori kisha wakafunga macho na kusali.
********
Haukuwa utani wala kanjanja,kazi ya Leila ilikuwa ni moja, kuhakikisha Deo anatoka gerezani kwa gharama yoyote ile na jinsi alivyosikiliza kesi yake aliamini kuwa ana uwezo wa kumtoa gerezani kwa njia ya kukata rufaa na kuomba kesi ichunguzwe upya,alifanya hivyo kwa moyo mkunjufu kabisa.Na jinsi alivyokuwa anafahamiana na watu ilikuwa rahisi sana kuonana na wanasheria.
“Mtafute advocate mmoja anaitwa Elifazar Mdassa,ni professional.Ofisi zao zipo pale Kinondoni,mwambie mimi nimekutuma.Namba zake ni hizi hapa”
“Thanks Gerald,Be blessed”(Ahsante Gerlad ubarikiwe)
Siku hiyo hiyo Leila alikodi taxi baada ya kupashwa habari juu ya mwanasheria huyo ambaye alipewa sifa zake,ndani ya dakika kumi na sita baadaye alikuwa nje ya ofisi za Engleas Nest Law advocates company,jina hilo la kampuni hiyo halikuwa ngeni masikioni mwake baada ya kuelekezwa kupitia simu.Akakaribishwa mpaka ofisini.
“Gerlad amenipigia simu ameniambia una matatizo”
Advocate Mdassa alianza mazungumzo,kwa harakaharaka umri wake ulikuwa kati ya miaka 40-49 lakini mambo yake yalikuwa mazito kuliko kawaida.Elifazar Mdasa katika historia yake tangu asome sheria hakuwahi kushindwa kesi kirahisi,ndiyo maana jina lake lilivuma kwa kasi ya roketi!
“Mimi naitwa Elifazar Mdassa”
“Leila,call me Leila”(Niite Leila)
“I’m listening”(Nakusikiliza)
Leila akaanza kuongea kila kitu na katika maongezi yake akamtaja Deo Karekezi,akamwambia kila kitu kilichotokea mpaka rafiki yake akafungwa!Advocate Mdassa alikuwa makini mikono yake ipo chini ya kidevu anamsikiliza Leila.
“Kwahiyo alivyouza hiyo saluni ndipo akapewa pesa feki?”
“Ndio”
“Alivyopeleka benki,wakamkamata?”
“Ndiyo”
“Sasa nani alifungua mashtaka,alikuwa ana upande wa mashahidi?”
“Hilo sina uhakika lakini nyuma ya hayo yote,kuna watu walikuwa wanamdai.Ndiyo wakamkandamizia hapohapo”
“Ngoja kidogo,hapo kwenye pesa feki kwanza.Ndiyo swala zito!Walimkamata na kithibiti chochote mbali na hizo pesa?”
“Sidhani”
“Anyway ningependa kwenda kuzungumza na Deo mwenyewe huko gerezani lakini kwa sasa hivi inabidi iandikwe barua iende mahakama ya Rufani.Nipewe Go ahead ya kutoka kwa Jaji aliyehukumu kesi yake,iandikwe shauri.Kwa uzoefu niliokuwa nao hapo asilimia sabini,atatoka jela!Cha kufanya wewe jipange”
Advocate Mdassa alizungumza kwa kujiamini sababu alijuwa ni kitu gani anachokifanya na alivyoagana na Leila hapohapo akaanza kuandika barua ili aitume mahakama ya Rufani,ili kesi ifufuliwe upya.
“Sporah Tajieli,tuma hii barua kwa Jaji Barnabas Kodende sasa hivi”
Mfanyakazi mwingine ambaye alikuwa ni sekretari,akapewa barua baada ya dakika thelathini kupita na muda huohuo ikatumwa kwa njia ya mtandao yaani ‘email adress’.
“Tayari”
“Ahsante”
Advocate Mdassa akashusha pumzi ndefu kidogo, akisubiri mrejesho kutoka kwa Jaji Kodende ili aanze mchakato wa kazi yake mara moja!




Harakati za ukombozi zilianza mara moja kwani maswala ya kuendesha kesi mpaka gharama za kumlipa mwanasheria,kesi kuanzishwa tena upya,zilikuwa chini ya Leila na jukumu hilo alijitwisha mwenyewe bila kulazimishwa na mtu wa aina yoyote ile,alifanya hivyo sababu ya huruma aliyokuwa nao moyoni hata hivyo kwa mabaya yote aliyomfanyia Deo ilibidi amridhishe kwa kumfanyia wema,alikuwa ana kila sababu za kufanya hivyo kwani bado hakuwa ana uhakika kama Deo alimsamehee kutoka ndani ya mtima wake.
Aliamini kitendo cha kwenda gerezani kuongea na wafungwa ilikuwa ni kama Malaika wa Mungu alimuingia na kumwambia afanye hivyo ili akutane na Deo Karekezi,hivyo ndivyo imani yake ilivyomtuma.
Kila asubuhi,Leila alilazimika kwenda kwenye ofisi ya Advocate Elfazar Mdasa ili kujua mpango mzima wa kesi utakavyokuwa.
“Inabidi kwanza nionane na huyo Deo Mwenyewe ili ainelezee ilivyokuwa.Tayari nishakata rufaa.Na good thing,mimi ndiyo nitakuwa wakili wake kama hutojali”
“Mimi sina shida yoyote ile”
“Utaingiza mzigo wangu kwenye namba ya akaunti niliyokupa,next week uje na bank slip za malipo”
“Sawa Ahsante”
“Karibu tena”
Maongezi hayo yalihitimishwa, na Leila alisimama na kutoka ofisini ambapo baadaye alienda moja kwa moja kupakua pesa na kuziingiza kwenye akaunti ya CRDB kwa ajili ya malipo.Kwakuwa alikuwa amerudiana na mzungu wake wa Uingereza,swala la pesa halikuwa tatizo kwake,alivyomaliza taratibu zote alirudi nyumbani kwake na kuanza kumuomba Mungu wake aliye juu mbiguni afanye miujiza kwani alijuwa pasipo yeye hakuna jambo lolote lile ambalo lingeendelea.
Hatimaye siku ya kuwaona wafungwa ikafika,watu walikusanyika gerezani ili kuwaona ndugu, jamaa na marafiki zao waliokuwa na vifungo gerezani,hiyo ndiyo siku ambayo Leila alienda na mwanasheria.Ujio huo, ulimshtua sana Deo kwani jambo kama hilo hakulitia maanani, hata kidogo.
“Deo,huyu ndiye advocate ambaye atakusaidia kwenye kesi yako.Anaitwa Elfazar Mdassa”
Leila akaanza utambulisho na pembeni yake kushoto alikuwa ameketi Mr.Mtui,wakamsabahi pia!
“Nashukuru kukufahamu”
“Leila amenielezea kila kitu kuhusu kesi yako.Na nilipofikia tayari nimekata rufaa ili uchunguzi uanze upya.Nadhani upo tayari kuonesha ushirikiano wako Mr.Deo”
Maneno hayo aliyazungumza Advocate Mdassa huku akitoa nyaraka mbalimbali za mahakamani na barua ambayo ilitolewa na Jaji Barnabas Kodende,bado Deo hakuamini kilichokuwa kinataka kutokea mbeleni.Hata hivyo alikubali na kuonesha ushirikiano wa kila kitu,hakuacha neno hata moja nyuma,alizungumza kila kitu kilichotokea tangu alivyopewa tenda ya vifaa vya ujenzi na mara ya mwisho alivyouza saluni yake,akabambikiwa pesa bandia.Alivyokuwa anazungumza hivyo, Mdassa yeye alikuwa makini sana kuandika kila kitu juu ya karatasi yake maalum.
“Baada ya hapo?”
“Nikakamatwa benki,nikapelekwa msimbazi.Nilichanganyikiwa alafu mbaya zaidi nilipaniki sababu mali zangu zote zilipigwa mnada”
“Kuna uchunguzi wowote ule uliofanyika,walikukuta na huo mtambo wa kutengeneza pesa feki?”
“Hapana,sikuwa na huo mtambo wala sikuwahi kufanya biashara haramu tangu nizaliwe.Lakini kilichonikandamiza sana ni yule dada wa kihindi aliyekuwa ananidai”
“Tuseme yeye ndiye aliyepigilia hiyo kesi msumari?”
“Ndio,akidai kuwa nilitaka kumdhulumu.Nilivunja naye mkataba na alikuwa yeye na mumewe pia”
“Well,hao watu uliowauzia saluni unawafahamu?”
“Hapana,walinipigia tu simu sababu niliweka tangazo kwenye gazeti”
“Ulitumia mtandao gani kuwapigia?”
“Tigo na Airtel”
“Thank you,niandikie namba zako za simu hapa juu”
Mtui na Leila walikuwa makini kusikiliza mahojiano kati ya Deo na Mwanasheria huyu aliyekuwa ana maswali mengi kuliko polisi,baada ya mahojiano hayo ambayo yalikula muda wa dakika arobaini nzima,Advocate aliaga na kuhaidi kuwa atafanya uchunguzi wa chini kwa chini ili kesi hiyo ifufuke na uchunguzi uanze upya,kulikuwa kuna kila dalili ya matumaini ya kesi kushinda na hivyo ndivyo hata Leila alimuhakikishia Deo Kerekezi.
“Utatoka Deo.Mkeo yuko wapi?”
Leila aliuliza kwani kutokuwepo kwa Marietha kulimfanya ahoji.
“Yupo”
“Msalimie sana,natamani nimuone!Siku hizi kanisani haji tena,usharika unamuulizia kila siku.Sidhani kama kuna watu wanajua upo mahali hapa”
“Haina haja ya kumwambia mtu yoyote yule”
“Sawa”
“Leila,ahsate kwa kila kitu”
“Usijali”
Hivyo ndivyo ilivyokuwa.

***********
Maisha ya Marietha yalikuwa ya raha mustarehee,hakuwa tena na shida katika maisha yake na tayari alikuwa keshaupiga umaskini teke,kila kitu kwake kilikuwa bomba na alikuwa akibadilisha magari ya kifahari kama nguo leo Range,kesho Landcruiser vx,kesho kutwa atatembelea BMW!Alikuwa akiishi kwenye nyumba kubwa yenye kila kitu ndani yake,wafanyakazi kila kona,kifupi nyumba yake ilikuwa kama pepo ndogo kwani aliamini ndivyo peponi watu wanaishi kama yeye, sababu hakuna kitu ambacho alikosa kutoka kwa Mzee Maximo,watoto wake aliwaanzisha shule kubwa ya matajiri ambao wazazi wenye uwezo ndiyo waliodiriki kuwaanzisha watoto wao shule hiyo.
“Baby,nitasafiri tena”
“Wapi tena mpenzi wangu?”
“Nitaenda London,nina kikao”
“Utaenda lini?”
“Nitaondoka na ndege ya usiku wa leo”
“Baby,kila wakati una safiri.Mimi ninakuwa mpweke tena”
“Inabidi iwe hivyo ili tutengeneze maisha,bila kusafiri usingekuwa unaendesha magari na kukaa ndani ya nyumba kama hii.Ni lazima nikafanye kazi”
“Utarudi lini baby?”
“Nitakaa siku tano Mpenzi wangu”
Siku hiyo Mzee Maximo alikuwa juu ya kitanda,Marietha yuko kifuani kwake anachezea kitambi na kifua cha mzee huyu tajiri,hakuamini kama maisha kwake yamekuwa ya namna hiyo na wakati mwingine alijuta kabisa kuolewa na Deo Karekezi.
Usiku wa siku hiyo, Mzee Maximo alisindikizwa uwanja wa ndege na safari ya kuondoka ikawadia akimuacha Marietha nyuma,anasononeka!Wanaume waliokuwa wanamuona Marietha walimtamani lakini hakuna hata mmoja wao aliyethubutu kumtongoza,walihofia uhai wa maisha yao kwani walimuogopa sana Mzee Maximo na habari za Mzee Maximo kutoka na Marietha kimahusiano zilisambaa kwa kasi ya kilomita mia kwa sekunde.
Ilikuwa ni bora ucheze na pesa ama mali zake kuliko kucheza na wanawake zake.Maximo alikuwa ana tabia ya kuteka watu na kuwaua kama akihisi mtu anakula naye tunda moja,kitu kilichofanya mpaka walinzi wake wamuogope mzee huyu ni baada ya kumfuma mkewe anafanya mapenzi na dereva wake,alichomfanya ni kumkatakata vipisi vidogovidogo kama mishkaki kwa mikono yake kisha mkewe huyo alimpiga risasi ya kichwa hapohapo,miili ya watu hao ikaenda kutupwa Ziwa Tanganyika, jamaa na marafiki waliwatufa ndugu zao mpaka wakachoka lakini hawakufanikiwa kuwapata hakuna hata mtu mmoja kati yao aliyejuwa watu hao waliuwawa na Mzee Maximo, yeye pamoja na gaidi mmoja aliyemuita ‘Black Ninja’ chochote kibaya kikitokea ama akidhulumiwa mali zake basi hushtaki kwa Balck Ninja, akifanya hivyo basi kila kitu kinaenda shwari,huo ndio ulikuwa upande wa pili wa shilingi wa mzee huyu!

****** *****
“Darling,kuna barua hapa nimeletewa imetoka mahakamani”
“Barua ya nani?”
“Embu isome”
“Nipatie”
Siku hiyo usiku baada ya Dokta Katrina kurudi nyumbani kwake, alikumbana na barua kutoka mahakamani na chini ilitiwa sahihi ya mwanasheria Elifazar Mdassa!Ikiwataka mahakamani mwezi mmoja baadaye tarehe 22,jambo hilo lilimshtua Issa, akiwa anamalizia kuisoma.
“Ndio ile kesi ya Deo?Yule tapeli wa kimataifa?”
“Hiyo hiyo”
“Ha! Ha! Ha! Haaaaa!Wanataka kufanya nini?Embu wasinisumbue, mwache akae kwanza gerezani miaka yake kumi na tano ili adabu imkae vizuri”
“Lakini lazima tutii huu wito,hii barua ya jamhuri ya muungano wa Tanzania”
“Utaenda mwenyewe”
“Baby”
“Mimi nitasafiri alafu Karishma amelala?”
“Alikuwa seblen,nadhani keshalala sasa hivi”
Karishma, ndilo jina la kihindi walilompachika mtoto wao huyo wa kike,chotara!Alikuwa ni mtoto mrembo kisawasawa, rangi yake ya mchanganyiko ndiyo ilikuwa tishio kubwa sana, watu wengi waliomuona mtoto huyo wa kike walimtabiria kuwa ni lazima angekuwa Miss World miaka ya baadaye,maana uzuri wake haukuwa na mfano wa kuufananisha,mbali na hapo alipewa matunzo mazuri kwani wazazi wake walikuwa wenye uwezo kifedha!Ingawa kulikuwa na basi la shule lakini Karishma alipelekwa na gari la nyumbani na kurudishwa na dereva maalum aliyeajiriwa kwa kazi hiyo,mtoto huyu aliongeza upendo kwa wanandoa hawa wawili.
“Maendeleo ya Hoteli vipi?”
“Huko salama mambo si haba.Ndio nimeanza project na kutengeneza Parking ya magari”
“Well baby,ndio maana nakupenda sana.Upo smart sana kichwani”
“Etii eeh,kwani ulikuwa hunipendi?”
“Umeanza sasa”
Issa na Katrina walipendana na hakuna hata mmoja kati yao aliyekuwa tayari kutenganishwa na binadamu yoyote yule isipokuwa kifo tu,upendo wao pia walimpandikizia mtoto wao mdogo wa kike aliyeitwa, Karishma!
*******
Baada ya kupewa vibali vya kufuatilia kesi, Advocate Elfazar Mdasa, alinyooka moja kwa moja kituo cha polisi oysterbay ili kupewa barua ya kwenda taasis ya Mawasiliano Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA), kwa ajili ya kwenda mitandao ya kampuni ya simu TIGO na AIRTEL,hakukuwa na muda wa kupoteza baada ya kufika Makao makuu Tigo na kueleza shida yake.
“Tupatie namba zake mara moja”
Mkurugenzi mkuu katika kitengo cha mawasiliano cha huduma kwa wateja, aliyeitwa Elizabeth Mrosso ndiye alikuwa nyuma ya Kompyuta na kuanza kazi ya kuandika namba za simu.
“Barua inasema unahitaji mazungumzo na simu zilizopigwa na simu zao”
“Kila kitu kimeandikwa hapo”
“Sawa”
Dakika thelathini zilikuwa nyingi, mazungumzo yote yalikuwa tayari yapo mezani na hiyo ilimfanya Adovocate Mdassa asikilize kila kitu.
“Naomba namba za huyu aliyekuwa anazungumza na Deo pia, nijue ruti zake zinapatikana wapi”
“Hii namba imeacha kutumiwa muda sana”
“Naweza kujua mara kwa mara huwa anazungumza na nani?”
“Ndio,nipe dakika tano”
Bongo ilikuwa kama Ulaya vile,kwa jinsi teknolojia na utandawazi ulivyokuwa kwa kasi, haikuwa rahisi kucholopoka kama ungevaliwa njuga,hivyo ndivyo alivyofanya Advocate Mdasa na kupitia mtandao wa simu, ilikuwa rahisi kumkamata muhalifu huyo ambaye alimbambikia Deo Karekezi pesa bandia.
“Mara ya mwisho alimpigia mtu anayeitwa Happy Massamu na huyu ndiye pia simu yake inaonesha mara kwa mara walikuwa wakizungumza”
“Namba yake inapatikana?”
“Subiri tena….Ndio ipo hewani na inasoma mnara wa Kinondoni,Dar es salaam”
“Ahsante”
Kazi yake ikawa imeishia hapo hakuwa na haja ya kutumia nguvu za aina yoyote ile,ni akili tu kichwani ndizo zilizokuwa zinachaji.
Alivyotoka hapo, akapitiliza moja kwa moja kituo cha polisi cha kati na kuchukua RB ya mwanamke huyo huku akiomba askari wengine watatu ili Happy Massamu atiwe mikononi mwa sheria na huyu ndiye angetaja ni wapi tapeli huyo anapatikana.
Swala hilo lilifanyika ndani ya siku mbili na nusu,Happy Masamu akawekewa mitego na maaskari,akajaa ndani ya boxi akawekwa chini ya ulinzi,akakokotwa mpaka kituoni.Kutokana na hofu kumtanda ilibidi ashirikiane na polisi, awe nao bega kwa bega!
“Hii ndio itakuwa tiketi yako ya kuwa huru binti,usipofanya hivyo utanyea debe.Tunamuhitaji huyu mtu kwa usalama wako”
“Sawa afande,nipo tayari”
Mpango ulisukwa siku hiyohiyo, Happy Massamu akafanywa chambo,akawekwa mstari wa mbele ili afanikishe zoezi hilo,siku hiyohiyo usiku polisi walimpata muhalifu wao na kwa bahati nzuri wakamkuta na mtambo huo wa kutengeneza pesa bandia,hakukuwa na cha msalia mtume akapigwa pingu.
Siku inayofuata Advocate Mdasa akachapa barua na kuwatumia wafungua mashtaka Katrina na Issa ili baada ya mwezi mmoja wafike mahakamani kwa ajili kusikiliza tena kesi upya,kwake swala hilo alilichukulia ni ushindi tayari.
*** ******
Bata la Marietha alilokuwa anakula halikuwa la kawaida na aliweza kuzitumbua pesa za Mzee Maximo sawasawa,alijiona yeye ndiye yeye na maisha ametusua, hakuna kiumbe yoyote atakayeweza kumsumbua awe wa nchi kavu au baharini.
Sio siri alizidi kupendeza na kunawiri, ngozi yake ikawa nyeupe pee!Akawa maarufu ghafla kupitia mgongo wa Maximo na kila alipoenda kununua nguo dukani alikumbana na usumbufu kutoka kwa wanaume ambao hawakutambua kuwa alikuwa ni awara wa Mzee Maximo.
“Kaka,kama unataka kutekwa embu jaribu kumtongoza huyo mwanamke.Hujitakii mema wewe”
“Wapiii wewe,nzi kufia kwenye kidonda sio ufala ni kupenda.Kwanza nani aniteke?”
“Unamjua Maximo wewe?Kama hutaki kuliona jua la asubuhi jaribu tu”
“Subiri uone huyu mtoto mimi nampiga miti.Namdinya nakwambia”
“Kipumbu!Kipumbu!Kipumbuu! achana na huyo mwanamke”
“Subiri nikuoneshe kuwa mimi ni mtasha sisi ndio wazawa,downtown kitambo jembe langu.Huyu Marietha sijui nani,nampiga dudu.Na ninakwambia kuwa hachomoi nitakuwa nalelewa,si unajua mimi kitandani sikosei.Kama Ronaldo”
“Utanikumbuka Kipumbu,achana na huyo gashi”
Yalikuwa ni malumbano ndani ya duka moja la Nguo ambapo hapo kila mwisho wa wiki Marietha alifika kununua nguo zake na za Maximo pia,katika watu waliotokea kufa na kuoza ni kijana huyu sharobaro aliyeitwa Kipumbu, hakujuwa kumfukuzia Marietha ilikuwa ni sawa na kujichimbia kaburi.
Jitihada zake alihisi zilianza kuzaa matunda kwani alifanikiwa kupata namba za Marietha na kila siku alikuwa akimpigia simu, wanaongea usiku.
“Kwani wewe Marietha Team Kiba au Mondi?”
Siku hiyo Kipumbu alianza gia zake kwani alishajua Marietha anapenda sana nyimbo za Bongofleva,alitaka kutumia mwanya huo kumvua samaki wake!
“Mimi nampenda Diamond lakini Ali kiba pia anajua kuimba”
“Chagua mmoja”
“Diamond”
“Nyimbo gani ya Diamond ambayo unaipenda?”
“Inaitwa Kesho”
“Sasa ile nyimbo nzima mimi nimemvalisha na mimi ndiyo nilimwandikia mistari pia,pale inapoanza anavyosema Zachaa.Sasa huyo Zacha ni kaka yangu”
“Diamond unamfahamu kweli?”
“Mpaka Mama yake,Bi.Sandra namjua.Au nikupeleke siku ukamuone?”
“Mh,aya tutaangalia”
Kwa asilimia fulani bwana Kipumbu, alijiona ni mshindi na alifanikiwa kuichukua akili ya Marietha,mambo ya mziki yalivyoisha aliingizia slogan za Bongo movie, akajifanya anamjua JB,Ray,Anti Ezekiel na akina Irene Uwoya.
Akazidi kumsogeza karibu na hapo ndipo alipoanza kujielezea hisia zake na ndilo kosa alilofanya kwani baada ya kumtamkia Marietha kuwa anampenda, siku iliyofuata hakusikika tena simuni, ikawa kama masihara lakini ndiyo hivyo Kipumbu akawa amepotea katika mazingira ya kutatanisha,huo ndio ulikuwa mwisho wa Kipumbu.

Jambo hilo lilimuumiza sana Marietha lakini aliogopa kumuulizia kwa marafiki zake! Siku moja baada ya mwaka kupita akiwa ndani ya jumba lake kubwa alilohongwa,alishtuka baada ya kuona namba ngeni juu ya kioo chake cha simu,akaipokea na kuiweka masikioni.
“Halloo Marietha…mimi Deo Karekezi Mumeo hapa Baba Abraham.Huwezi kuamini kuwa nimetoka gerezani nipo huru sasa.Njoo kwa Mtui mke wangu,nimekumisi sana.Sipati picha nikikuona,uko wapi nije?”
Moyo wa Marietha ukapiga kwa nguvu kusikia sauti hiyo,akatoa simu sikioni na kuangalia tena kwani hakutaka kuamini, alichokisikia kilikuwa ni kweli ama kasikia vibaya!




Ilikuwa ni mnamo terehe 19,July.Watu wengi sana, walikusanyika mahakamani ili kusikiliza kesi hiyo ambayo ilikumuweka Deo Karekezi gerezani kwa kosa la kukutwa na pesa bandia,kwake akiwa kizimbani alijifananisha kama mtu anayecheza kamali kupuna ama kukosa,hakuwa na matumaini kabisa ya kutoka gerezani baada ya kusota miaka minne na miezi nane ingawa alimuomba Mungu aweke mkono wake na awe huru, kwani maisha ya Gerezani kwake yalikuwa ni sawa ya Jehaman!
Nyuma ya kesi hiyo na watu waliokuwa chachu ni Issa Nurdin Mpelembe pamoja na Mkewe Katrina,hawa ndiyo waliosimama upande wa mashahidi na walikuwa wapo makini kusubiri zamu yao ya kupanda kizimbani.Kitu hiko hakikumtingisha Advocate Elfazar Mdasa wala Leila kwani waliamini moja kwa moja ushindi ulikuwa wao,Mahakama ilikuwa na ukimnya wa ajabu, hakuna hata mtu mmoja aliyeongea.
“Kortiiiiiiiiiii”
Mahakama nzima ilisimama kwani Majaji pamoja na mawakili walikuwa wakiingia kisha kuketi kwenye viti vyao mbele kabisa,hapohapo kesi ya Deo ikaanza kusikilizwa tena kwa mara nyingine!Upande wa washtaki wakaanza, akapanda Issa Nurdin Mpelembe na kuongea kila kitu na vitu vingine aliviongezea kwani hakuwa tayari kumuona Deo Karekezi anakuwa huru,kuna vitu vilimtia hasira sana huko nyuma.
“Ni kweli ana pesa feki na mfanyabiashara haramu,alitaka kumpa mke wangu pesa feki.Ni tapeli, alitutapeli mamilioni ya pesa”
Issa alizungumza huku akimtizama Deo kwa hasira na wakati mwingine alikuwa akimwangalia Advocate Mdasa aliyekuwa amesimama mbele yake kanyonga tai nyeusi,shati jeupe anamsubiri kwa usongo amalize anachokiongea kisha amtwange maswali,yasiyokuwa na idadi kamili.
“Issa Nurdin Mpelembe,unasema mteja wangu ni mfanyabiashara haramu,unaweza kuidhibitishia mahakama tukufu kuwa una ushahidi huo?”
Issa alitandikwa swali!
“Sina moja kwa moja lakini ushahidi ninao, kutengeneza pesa feki ni kucheza na nyaraka za serikali,huyu hastahili kuwa hapa.Angekuwa huko nchi za kiarabu, angenyongwa”
“Una miaka mingapi bwana mdogo?”
“Wewe miaka yangu haikuhusu,uliza kinachotufanya tuwe hapa”
“Sawa,wewe unatetea nini hapa?Kuzulumiwa mali ama pesa bandia?”
“Kuzulumiwa mali na pesa feki,vyote”
“Mahakama yangu tukufu.Ninyi mlikuwa mnamdai Mteja wangu kiasi cha shilingi milioni mia moja themanini pamoja na faini ya kukata mkataba ikawa shilingi milioni mia mbili na themanini.Lakini wewe ukauza mali zake zote ambazo thamani yake ni shilingi milioni mia nne na sabini.Ukafanya siri na kugushi sahihi wewe na mwanasheria wako bila mkeo kujua,una iambia nini mahakama leo hii?”
Issa Nurdin Mpelembe, alihisi mkojo unataka kumpenya, hakuelewa ni kivipi Advocate huyu Mdasa amefahamu siri hiyo kubwa ambayo hata mkewe hakuwa ana habari nayo,hilo ndilo lililompagawisha zaidi na zaidi.
“Hu…o huo huo ni uwongo kabisa”
“Subiri”
Advocate Mdasa hakubahatisha kwa kitu anachokifanya,akatembea mpaka kwenye meza yake na kutoa karatasi,moja ilikuwa yenyewe halali na nyingine bandia pamoja na mali zote za Deo na thamani zake na jinsi hisa za kampuni zake zilivyouzwa kupitia barua ya kugushi,hiyo ilimshtua sana Katrina aliyekuwa amekaa upande wa washtaki lakini katika nafsi nyingine ilimwambia kuwa hapana haikuwa kweli,jambo lililozidi kumuogopesha ni baada ya kumuona Issa ana haha kujibu maswali,akabaki kimnya anasikiliza kile ambacho ataenda kujibu.
“Hapa ulidhulumu, na hii sahihi uligushi kwa bwana Juma Matobosa pale Posta tarehe saba mwaka huu hapa.Kataa leo mbele ya mahakama.Ni hayo tu bwana hakimu,ahsante”
Advocate Mdassa aliendelea kumtetea mteja wake na baadaye akaibuka na sauti ambazo Deo alikuwa akiongea na mteja ambaye walifanya naye mawasiliano,mpaka akapachikiwa pesa bandia,hiyo ilimshangaza kila mtu.

Kila kilichotokea mbele ya Deo ilikuwa ni kama Sinema vile na matumaini yake yalianza kurudi upya,ghafla picha ya Marietha ilianza kumjia akiwa na watoto wake akiwa yupo huru.Kesi haikuwa ngumu kwani ushahidi ulikuwa wazi kabisa,Meno ya Leila yote yalikuwa nje na muda wote alikuwa akitabasamu,Mtui na mkewe ndiyo usiseme, furaha yao ilionekana waziwazi kabisa.Majibishano yalivyokuwa yanaendelea makarani walikuwa na kazi ya kuandika kila kitu, hatimaye kesi ikarushwa mwezi mmoja mbele ili hukumu itolewe na jaji huyu Barnabas Kodende!
Baada ya kesi tu kuisha, ugomvi mkali uliibuka kati ya Katrina na Issa kuhusiana na dhuluma zilizotokea nyuma yake,Katrina alishangaa na hakutegemea kama Issa angefanya jambo la dhambi namna hiyo!
“Kweli tabia ni ngozi ya mwili kamwe huwezi kuibadili”
Katrina aliropoka, akiingizia msamiati huo huku akiangalia pembeni,jambo alilolifanya Issa lilimkera na kumtia kichefuchefu kwa ujumla.
“Issa unafanya dhuluma,sitaki kuamini?”
“Laki..”
“Lakini nini?Shut up…Shut up..Sitaki kusikia ujinga unaotaka kuniambia,sitaki kabisa!Nishajua tabia zako tayari”
“Katrina nisikilize sasa..”
“Nikusikilze nini sasa wakati ushaiba,pesa ziko wapi?Nataka urudishe pesa za watu mimi sipendi dhuluma kabisaa”
“Katrina nisikilize kwanza hiv..”
“Usiniambie chochote”
Ndani ya gari Katrina aliuwasha moto sio kitoto,akawa mkali kuliko pilipili mbuzi.
“Issa ni kweli wewe wa kufanya hivi?Wewe wa kunifanyia mimi hivi?Sitaki kuamini hata kidogo”
“Katrina nisikilize nachokwambia,punguza jazba”
“Siwezi kupunguza hata kidogo,umenikera mpaka basi.Kumbe hata siku ile ulivyoniambia kuwa kuna shoti ya milioni saba ulipiga dili sio?Mwizi kumbe wewe”
Katrina alitibuka kama maji kwenye bwawa,alichefukwa kupita kiasi na hakutaka kumuona Issa mbele yake,alimchukulia kama tapeli.Hiyo ilifanya mpaka Issa akae kimnya na kushindwa kuongea sababu ni kweli alitenda kosa hilo la dhuluma kwa Deo tena kimnya kimnya,alipiga pesa ndefu kupita kiasi.Na katika watu walioshinikiza kwa Deo kufungwa ni mwanaume huyu Issa aliyekuwa na kisasi kutoka ndani ya moyo wake!
“Issa wewe ni mtu gani, eeeh?Lini umeanza hii tabia?”
Katrina bado aliendelea kuongea tena.Moyo wake ulimtuma aseme na kutoa dukuduku alilokuwa nalo moyoni.Issa hakujibu chochote kwani aliendelea kuendesha gari bila kumjibu chochote kile,alimuelewa Katrina akianza kuongea anakuwa kama redio iliyowekwa mabetri mapya ya ‘National’na ndivyo ilivyokuwa kwani hata walivyofika nyumbani, Katrina aliendelea kumlaumu Issa kwa kitendo alichokifanya.
“Rudisha pesa za watu,nahitaji ufanye hivyo, tapeli wewe.Kwanini umefanya hivyo lakini?”
“Naongea nawewe Issa”
“Sasa nikitaka kuongea wewe hutaki,unataka nifanye nini?”
“Hata ukiongea utaongea nini?Wakati ushafanya dhambi.Sikutegemea kama umekuwa mshenzi namna hiyo,kwanini uridhiki sasa?Kama una shida ya pesa kwanini usingeniambia”
Katrina alizidi kuongea na kupaza sauti akizunguka chumba kizima,hiyo ilifanya mpaka Issa ajisikie aibu na hapohapo alikiri kosa na kuomba asamehewe kwani alifanya hivyo ili kulipa kisasi.
“No Issa,Revenge doesn’t change a past”(Hapana Issa,kisasi hakibadili yaliyopita)
“I’m so sorry,bado moyo unaniuma sana Mke wangu”
“Deo ana watoto lakini ana mwanamke anateseka mitaani huoni hata huruma?Hata kama mlishea mwanamke mmoja.Haipaswi,haifai wewe uwe hivyo,Mambo yaliyopita yamepita Mme wangu.Hakukuwa na haja yawewe kufanya ulichofanya,aya sasa mbele ya mahakama umeonekana tapeli,tena mbele ya Mama yangu.Unadhani atanifikiria nini?Nina mume wa aina gani?Stile up”
Katrina alizidi kutoa husia na somo kama mwalimu wa darasani, aliongea kisomi na kumwambia Issa ukweli wote kutoka ndani ya moyo wake.
“Naomba upige hesabu kiasi gani anadai,tuilipe na tafadhali naomba umuombe Msamaha ili maisha yaendelee”
“Sawa nitafanya hivyo,lakini nitaanzia wapi mke wangu?Naona aibu”
“Niachie mimi,nitajua namna ya kufanya ikifika kesho unipe hesabu za pesa hizo”
“Sawa Darling”
Hivyo ndivyo wanandoa hawa walivyokubaliana ingawa ilikuwa vigumu kwa Issa kufanya hivyo,moyo wake ulikuwa bado ni mzito kumtafuta Deo na kuomba suluu yaani matatizo yao wayaweke kando,kwake ulikuwa ni mtihani mzito sana,historia yake na Deo ilikuwa nzito na alivyokumbuka hayo alijisikia uchungu sana!Mara ghafla akakumbuka kipondo, alivyozolewa Manzese kama mwizi na kuingizwa ndani ya diffenda,akapigwa virungu,mwili ukawa hautamaniki,akanyang’anywa mwanamke wake aliyempenda kuliko wote duniani.
“Deo alininyang’anya tonge mdomoni,siwezi kuomba msamaha labda sio mimi Isaa Nurdin,ngoja atoke gerezani nitume vijana wamfanyie vitu vibaya.Siwezi kuomba amani wakati wa vita,picha limeanza.Afe mimi nife yeye”
Hayo yalipita kichwani mwa Issa akiwa yupo juu ya kitanda na alitaka kufanya hivyo ili kulipa kisasi,hakuwa tayari kuona Deo ana amani hata kidogo!
*******
Hakuna mtu aliyekuwa tayari kuamini kama Deo angekuwa huru hata kidogo,ilikuwa ni shangwe kubwa baada ya Jaji kugonga nyundo mezani na kusema kuwa ‘Mahakama imekuachia huru hauna kosa lolote”Mahakama nzima ilisikika yowe kubwa hasa kutoka kwa Mtui na Leila,furaha ilimzidi Mtui mpaka akaanza kulia machozi ya furaha, walivyotoka nje walikumbatiana na kurukiana kama watoto wadogo vile na kuanza kuruka ruka.
“Deoooo,Siamini.Mungu ni mkubwa”
Maneno hayo yalimtoka Mtui huku akimpiga piga Deo mgongoni ambaye tayari alikuwa anamwaga machozi kama mtoto mdogo aliyefiwa na wazazi wake,alivyoangalia pembeni alimuona Leila, akamsogelea karibu.
“Ahsante sana Leila”
“Mshukuru Mungu,sio mimi”
Meno ya Advocate Elfazar Mdasa yalikuwa njenje, siku hiyo alimfuata Deo na kumpa mkono.
“Pole sana Mr.Deo Karekezi”
“Ahsante”
Kifupi siku hiyo ilikuwa ni furaha iliyozidi kifani.Wote wakaingia ndani ya gari la Mtui na safari ya kwenda nyumbani kuanza mara moja ambapo huko Mtui na Mkewe waliandaa chakula kizito,kwa heshima kubwa siku hiyo mbuzi mzima alidondoshwa pilau la nguvu likapikwa.Walimtengenezea Deo chakula kizuri.
“Bado siamini unajua.Marietha na wanangu wako wapi?Uliniambia utawapigia simu waje,wako wapi?Hawajafika bado?”
Deo akaibua mada katikati ya maongezi wakiwa mezani wanakula.
“Wapo njiani wanakuja shiba kwanza,watachelewa kidogo kufika.Wakati ule alikuwa bado hajapanda basi”
Mtui alidakia na kutoa jibu lakini mkewe alimkata jicho fulani la kumwambia aongee ukweli.
“Atakuja kweli?Nataka msimwambie kama nipo hapa,nimfanyie surprise.Atafurahi sana!Marietha ananipenda unajua,nampenda sana”
Maskini ya Mungu,Deo hakuelewa kama Marietha aliyemuacha miaka ya nyuma siye yeye kabisa na mambo aliyokuwa anaongea yalifanya Mtui na Mkewe wamsikitikie sana kwani walijuwa ukweli!
Mpaka inafika usiku wa saa tatu baada ya Deo kuoga na kuvaa nguo mpya, hakumuona Marietha na hakukuwa na dalili yoyote ile,ilibidi amfuate Mtui na kumuuliza tena.
“Bado hajafika?Au basi liliharibika njiani?Ulimpigia simu tena?”
Deo aliuliza maswali,ukweli ulikuwa wazi lakini Mtui hakuelewa ni wapi aanzie.Alielewa ni kiasi gani Deo angeumia mtima.Kwa maana hiyo, alitaka jambo hilo alishuhudie mwenyewe!
“Kwanini usimwambie ukweli sasa?Utamficha mpaka lini?”
Mke wake Mtui alidakia,sababu alimuonea sana huruma Deo.
“Ukweli gani Shemeji?Marietha kafanya nini?Amekufa?”
Deo akauliza,kauli ya shemeji yake ilikuwa na utata!
“Hapana hajafa,ngoja nikupe namba zake.Subiri kidogo”
“Sawa,nataka nimpigie niongee naye mwenyewe,sitaki tena kumfanyia Surprise labda atawahi kufika”
Mtui alisimama kutoka seblen na kuingia chumbani ambapo alimpigia moja kwa moja simu Michael Muganda na kutaka namba za Marietha kwani yeye hakuwa nazo,dakika moja baadaye akatokeza Seblen na kumpa namba hizo Deo pamoja na simu.
“Ngoja nimpigie”
Deo akatabasamu, moyo wake ukapiga mkambo,hakuelewa atamwambia nini Marietha baada ya kupokea simu,mwili wake ulikuwa ukitetemeka kidogo na alikuwa mwenye haraka!Upande wa pili wa simu ukaanza kuita,ilivyopokelewa akaanza kujitambulisha na kuongea bila breki.
“Deo?Deo yupi?Mbona mimi sikufahamu”
“Marietha mimi mumeo Deo Karekezi,Baba Abraham.Acha Masihara basi,nipo kwa Mtui hapa,umefika wapi?Umepanda basi gani Mama watoto..”
“Kaka umekosea namba”
“Ma…tititi”
Hapohapo simu ilikatwa.
“Mmh,Mtui huyu sio Marietha, itakuwa umekosea namba labda.Embu angalia namba vizuri alafu nipe simu”
Hata ingekuwaje, namba zingekuwa ni zilezile,bado Deo hakutaka kukubali kuwa aliyezungumza naye ni Marietha ingawa sauti ilikuwa ndiyo ile ile.
“Lakini sauti yake na Marietha zimefanana sana kweli dunia hii wawili wawili.Embu kagua namba zake vizuri,zile za zamani alibadili?”
Hiyo ilikuwa ni hali ya kujifariji na alitamani aambiwe kuwa ni kweli amekosea namba.
“Ngoja nikwambie ukweli mchungu Deo shemeji yangu,Mtui anaogopa kukueleza ukweli anahofia utaumia moyo.Marietha ni Malaya,hakufai.Na huyo uliyekuwa unaongea naye ndiye mwenyewe wala haujakosea namba za simu.Marietha alitembea na Michael mtoto wa Dada yangu,mpaka sasa hatujui alipo,alimtukana Mtui mbele za watu…”
Mtui alijaribu kumzuia mkewe asizungumze lakini alishachelewa tayari kwani alishamwaga mchele chini.Hiyo ilifanya mpaka moyo wa Deo ufe ganzi,yalikuwa ni maneno mazito kuyasikia na hakuwa tayari kuupokea ukweli wa jambo hilo,akamgeukia Mtui.
“Ni kwelii?Mtui ni kweli?”
Deo alihisi kama uti wake wa mgongo umepigwa na baridi la ghafla,ndiyo maana aliuliza mara mbilimbili.


Hata kama angeuliza swali lile lile, mara hata zaidi ya tilioni moja jibu lake lisingebadilika,ilikuwa ni wazi Marietha ni mchafu wa tabia na alisaliti penzi, jambo ambalo hakuwa tayari kulipokea, ndiyo maana alidiriki tena kuuliza swali hilo kwa mara nyingine.
“Mtui,hapana siwezi kukubaliana na wewe.Na watoto wangu wako wapi?Marietha kabadilika kweli?”
Deo Karekezi alirudia swali lile lile,hiyo ilikuwa ni mara ya ishirini na mbili kama kumbukumbu za Mtui zilikuwa zinahesabu maswali yake na aliuliza hivyo machozi yakiwa karibu na mboni ya macho yake,alitamani Mtui aseme ‘Hapana nakuzingua mshkaji wangu’Lakini ilikuwa ni tofauti kabisa na ukweli ukabaki kuwa ule ule.Mbaya zaidi mke wa Mtui alizidi kupigilia msumari wa nchi saba, hiyo ilifanya Deo azidi kuumia zaidi na zaidi.
“No Mtui,hata siku moja siwezi kumfariji mtu kwa uwongo bora nimwambie ukweli aumie.Hayo ndiyo maisha niliyolelewa nayo nikiwa mdogo”
Mke wa Mtui aliingizia misamiati yake akijaribu kutetea hoja yake.
Siku hiyo Deo Karekezi, alikesha Seblen mwenyewe akiwa ameshika simu anajaribu kupiga namba ya Mke wake wa Ndoa Marietha lakini haikupokelewa na mwishowe akaanza kutuma meseji mbalimbali za kuomba masamaha japokuwa hakuelewa ni kosa gani haswa amelifanya,mambo mbalimbali yalipita ndani ya ubongo wake akawa kama mtu anayeangalia sinema ya kihindi tena yenye kutoa machozi,bado hakutaka kukubali kuwa Marietha amemuacha.
Wakati mwingine alidhani yupo kwenye maigizo makali sana tena yeye akiwa Single Mtambalike na Marietha ni Irene Uwoya na baada ya dakika kadhaa wangeambiwa ‘cut’ na kama wangekuwa wanacheza filamu siku hiyo basi ingeuza duniani kote sababu Deo alikuwa analia ukweli,macho yake yalikuwa mekundu kupita kiasi!
“Lazima niende kesho Tanga,Lushoto”Deo aliapia na alimaanisha!
******
“MARIETHA MIMI MUMEO DEO KAREKEZI,BABA ABRAHAM.ACHA MASIHARA BASI,NIPO KWA MTUI HAPA,UMEFIKA WAPI?UMEPANDA BASI GANI MAMA WATOTO..”
“KAKA UMEKOSEA NAMBA”
Ndani ya chumba hiko kulikuwa na utulivu wa ajabu kuliko kawaida na juu ya meza kulikuwa na kifaa maalum kinachoitwa ‘Sound filter’ ni kifaa ambacho Maximo alikuwa nacho na alikiunga moja kwa moja na simu za wanawake wote ambao yuko nao kimapenzi,ilikuwa ni lazima aweke kidude kingine kidogo ndani ya simu ya wake ama mahawara zake bila wao kujua,hata Marietha siku ya kwanza alivyomkubalia siku iliyofuata alivyoingia bafuni kuoga aliweka kidude hiko kidogo ndani ya simu yake na kazi ya kidude hiko ilikuwa ni kunasa sauti za simu zote zitakazoingia,alkadhalika alikuwa ana kompyuta yake ambayo aliiunga kitaalam,hiyo ilichukua meseji zote za Marietha anazotumiana na mtu yoyote yule na kujihifadhi na kila usiku aliingia na kuangalia Marietha na wake zake wote walizungumzia nini,hiyo ndiyo njia aliyokuwa anatumia kuwanasa vijana wenye tamaa za fisi kisha kuwauwa,Mzee huyu alikuwa ni mwenye wivu kuliko wivu wenyewe.
Sauti ya Deo ikibembeleza pamoja na meseji alizokuwa anamtumia Marietha ziliamsha pepo lake la kutaka kuuwa,wivu ulimkaba mpaka shingoni,kilichomuuma zaidi ni kubaini kuwa Deo Karekezi ni mume halali wa Marietha.
“Black Ninja”
Hapohapo aliinua simu na kumtafuta Israel wake.
“Upo wapi?”
“Nipo barabarani”
“Hujalala?”
“Huwa silali muda wote nipo kazini”
“Kuna kazi hapa”
“Sema,nipo tayari”
“Njoo kwangu”
“Sawa”
Sura yake ilitisha kupita kiasi,jicho lake moja lilikuwa bovu,kwa umbo alikuwa ni mrefu kwenda hewani na alipendelea kuvaa kofia na miwani ya rangi nyeusi hata kama ingekuwa usiku wa manane,Black Ninja alikuwa ni mtu hatari mno!Na kuuwa kwake lilikuwa ni jambo la kawaida sana yaani ilikuwa ni sawa na kunywa supu hotelini,na katika historia yake tangu aanze kufanya kazi hiyo alishauwa zaidi ya watu elfu moja,hakukosea na wakati mwingine huondoka na vichwa vya watu,inasemekana kuwa mganga wake alimwambia kuwa ni lazima afanye hivyo ili asikamatwe na katika kufanya unyama huo, alikuwa ni mtu makini kuliko jambazi anayetaka kuvamia ikulu,kifupi aliuwa kwa uangalifu.
Siku hiyo,ilikuwa ni usiku sana akiwa ndani ya gari lake maeneo ya Mombo,alivyopokea habari hizo alizungusha usukani na safari ya kwenda kwa tajiri Maximo kuanza mara moja kwani kulikuwa na kazi ya dharura alitakiwa kuifanya,dakika arobaini na tano baadaye alikuwa tayari amefika nje ya jumba la Maximo ambapo aliishi yeye pamoja na wafanyakazi wake wawili tu,akiwa na walinzi peke yake.
“Naomba mtupishe”
Maximo aliwaambia walinzi wake baada ya Black Ninja kufika seblen.
“Hata wewe Donald”
Maximo akasema tena kwa mlinzi wake huyu wa mwisho kabisa,hapo walibaki wawili tu seblen!
“Wisky”
Maximo akasema huku akitembea kwenye kabati la pombe kali.
“Hapana mkuu”
“Well,kuna kunguni analeta shida kidogo”
“Unataka nimfanye nini?”
Maximio akageuka na kumuangalia Black Ninja kwa umakini kidogo na kupitisha mkono wake shingoni,kumaanisha kuwa amchinje!
“Usijali,nipe namba za simu”
“Hilo sio tatizo kabisa”
“Sidhani kama ataliona jua la Kesho”
Black Ninja alipewa namba za Deo na kuondoka zake,huko alifanya utafiti wake usiku huo huo ndani ya chumba chake na kugundua kuwa simu hiyo haikupigwa ndani ya mkoa huo wa Tanga,kibarua kingine kikaibuka cha kusaka minara ya Tanzania.
Ndipo alipogundua simu hiyo imetokea jijini Dar es salaam mnara wa Tegeta,hakutaka kupoteza wakati, akachukuwa begi lake lenye silaha kali na kulipakia ndani ya gari lake,cha kwanza ni kwenda kituo cha mafuta na kujaza ‘full tank’ kwa safari moja tu,kwenda kumuuwa Deo Karekezi, jijini Dar es salaam!

**********
Kitu usingizi ulikuwa ni hadimu kupatikana siku hiyo ndiyo maana alikesha akitafakari mambo mbalimbali yaliyotokea katika maisha yake,ni wazi kuwa yalikuwa yana historia kubwa na angewatafuta watunzi wakubwa nchini kama Frank Silaa ama Eddazaria G.Msulwa basi historia yake ingeuza nakala nyingi sana.
Yeye na Marietha walipitia mikasa mingi sana,na siku zote alivyokuwa gerezani aliomba Mungu atoke ili aungane tena na Marietha na waanze moja, hayo ndiyo yalikuwa matumaini yake, hata siku Jaji Kodende alivyogonga nyundo mezani, lakini matokeo yake mambo yalikuwea kinyume kama alivyotarajia,kifupi mambo yalikuwa nje-ndani.Jambo hilo lilimtesa na kumuumiza moyo,kwa wakati huo aliamini angekuwa na familia yake angepata mwanga mpya wa maisha yake!
Saa kumi na moja ya asubuhi ilimkutia seblen,hapohapo alikurupuka na kutembea mpaka mlangoni mwa Mtui,hakujali kama wangekuwa wanafanya tendo la ndoa ama la!
“Ngo! Ngoo! Ngooo! Ngooooo!”
Aligonga mlango na kusikilizia,alivyoona kimnya akagonga tena!
“Naniii?”
Mtui akauliza kwa sauti ya kukwaruza,iliyoonesha ametoka katika usingizi mzito.
“Mimi Deo”
“Deo?Sasa hivi asubuhi yote kuna nini ndugu yangu?”
“Nahitaji kuzungumza nawewe”
“Aya nakuja”
Kwa ndani alisikia kitanda kinanesa,baada ya sekunde tatu alitoka Mtui akiwa na taulo.
“Nini Deo?”
“Njoo tuongee kidogo”
Wote wakatoka mpaka seblen.
“Nataka kwenda Tanga leo”
Deo akafunguka bila kupindisha maelezo yake!
“Taaanga?Kufanya nini?”
“Kumuona Marietha”
“Nani amekwambia yupo Tanga?”
“Hata kama hayupo,nitajua alipo.Nitaambiwa alipo na ndugu zake.Tafadhali nisaidie nauli ndugu yangu,nitakulipa pesa zak…”
“No!No! No!No!Mimi nitakupa pesa,haina haja ya kusema hayo yote lakini kwanini usisubiri mpaka kukuche kabisa?”
“Hapana wacha niende sasa hivi”
“Ungekata basi na hizo nywele ili uwe smart angalau”
“Usijali,nisaidie nauli mengine niachie mimi”
Moyo wa Deo ulimsukuma akaonane na Marietha ana kwa ana, akiamini wenda atabadili maamuzi yake,licha ya yote hakuwa tayari kuamini moja kwa moja kuwa mkewe amebadilika kiasi kwamba anasema hamjui.Aliamini majibu ya maswali hayo yote angeyapata kwa ndugu zake huko Lushoto,Maduda.Mtui alivyoingia ndani na kutoka,alimkabidhi kiasi cha shilingi laki moja za kitanzania.
“Sasa simu hauna,tutawasiliana vipi?”
Mtui akaibua swali.
“Nitaandika namba zako kwenye karatasi,nikifika nitatafuta simu”
“Hapana ngoja nikuongeze elfu thelathini,utanunua simu na laini”
“Sasa sina kitambulisho,nitasajili vipi laini yangu?”
“Hapo sijui itakuwaje,ngoja nikupe kadi yangu.Ukifika tafuta simu nipigie ili nikutumie pesa”
“Sawa,ahsante Mtui.Mungu akuzidishie”
“Amen”
Mtui na Deo Karekezi walikuwa kama ndugu ingawa hawakuchangia Mama wala Baba, walitokea kuwa marafiki wakubwa wa kufa na kuzikana,ndiyo maana Mtui alifanya hayo yote kwa upendo kutoka moyoni mwake,kila kitu kilivyokamilika Deo alifungua mlango na kutoka nje ambapo huko alitafuta bodaboda na kupanda.
Bado hakutaka kukubaliana na hali aliyokuwa nayo,alilinganisha maisha yake ya nyuma na ya wakati huo na kutamani kulia,hakuamini kuwa leo hii anaomba mpaka nauli kwa mtu.
Pikipiki ilimfikisha mpaka Ubungo Terminal,hapo akatafuta basi akaingia ndani.
Muda wote moyo wake ulikuwa ukipiga kwa nguvu sana kwani alitamani afike Tanga,ajuwe ni wapi Marietha alipo, mbali na hapo alitaka kumuona mtoto wake, Abraham!
Mabasi yalianza kuchomoka, saa kumi na mbili juu ya alama,kutoka Ubungo, hapo Deo alikuwa akisali kwa Mungu wake ili afike salama!
*******
Black Ninja,jambazi hatari aliyetumwa na Maximo aliingia jijini Dar es salaam na gari yake binafsi saa kumi kasoro dakika nane, hiyo ni baada ya kuangalia saa yake ya mkononi,alifurahi kufika mapema namna hiyo kwani alimuahidi tajiri yake kuwa Deo hatoliona jua la asubuhi yaani siku inayofuata angekuwa mfu na mwili wake usingeonekana mahali popote pale yaani angepotea katika mazingira ya kutatanisha,hiyo ndiyo ilikuwa sifa ya Black Ninja,kuteka nyara kisha kuuwa na kuutupa mwili baharini ama wakati mwingine,aliichoma moto miili ya binadamu wenzake na ilivyogeuka majivu aliiweka ndani ya mfuko na kutupa jalalani.
Sio siri mtu huyu alitisha kuliko hata Dictator Adolf Hilter.Alivyofika Tegeta nyuki akaweka gari kando na kuangalia 'ipad' yake ambayo ilimuonesha kuwa mtumiaji wa Simu yupo eneo hilohilo,akavuta karibu na kugundua nyumba alipokuwa Deo Karekezi.
Hapohapo akarudisha gia mpaka kwenye herufi ‘R’akapiga norinda na kuliweka gari sawa akaingia barabara ya soko la Tegeta Nyuki,akazidi kusonga mbele, mpaka alipofika nje ya geti la rangi nyeusi.
“Ndio hapa”
Alisema hivyo huku akiwa anaangalia 'ipad' yake ambayo ilimuonesha kuwa bado mtumiaji wa simu yupo ndani,ambaye aliamini ni Deo Karekezi!Akauangalia ukuta harakaharaka na kupiga hesabu zake kichwani.
Akavuta begi lake lililokuwa na vifaa vyake vya mahangamizi,ambapo ndani kulikuwa na bastola ndogo,akavuta na kiwambo cha kupunguza sauti,akachukua na kisu kidogo kisha kukiweka kibindoni.
***********
Tangu Deo alivyoondoka asubuhi hiyo, Mtui hakupata usingizi tena, alichofanya yeye ni kumchokoza mkewe kimahaba ili apate unyumba,akaanza kumpapasa mwili mzima ili apewe.Bahati nzuri mambo yakajipa kwani mkewe alionesha ushirikiano akamsogelea karibu Mtui na kutoa nguo yake ya kulalia,wakaanza kushikana shikana.Mambo yalivyokuwa tayari Mtui aliipanua miguu ya mkewe na kupanda juu yake hapo aliingiza ndizi yake na kuanza kufanya tendo hilo, ambalo lilihalalishwa kwao,mpaka inafika saa moja kasoro walikuwa tayari wamemaliza tendo hilo,Mtui akasimama na kuingia bafuni ambapo huko alijimwagia maji, alivyotoka alikuta nguo tayari zipo kitandani, mkewe kamuandalia.Akavaa vizuri na kuweka tai vizuri,akachukua na koti la suti na kulitia mwilini,akaingiza mkono chini ya mto na kutoa bastola yake kisha kuiweka nyuma ya kiuno,akaifunika na koti.
“Baadaye basi,alafu Hoyce alinipigia jana,anasema uende kwenye ule mkutano.Utaanza saa kumi”
“Nitaenda.Alafu pesa sasa mbona hukunitumia tena jamani”
“Leo nakutumia Tigo pesa”
“Okay,mimi napumzika bado.Nikiwa natoka nitakwambia”
“Utaipitia na gari gereji pale kwa Shebi”
“Ayaa,kazi njema”
“Ahsante”
Mtui aliagana na mkewe,akatoka nje na kuingia ndani ya gari, ambapo kama kawaida yake kwanza alitoa bastola yake na kuiweka chini pembeni ya mlango,akawasha gari na kulirudisha nyuma,lilivyokaa sawa akaweka mkao wa kulitoa getini,masai akafungua geti.
Akatoa gari nje kwa safari ya kwenda kwenye kibarua chake.
*****
KITENDO CHA Landcruiser Vx, kutoka nje ya geti,black Ninja akawasha gari na kuanza kufuatilia gari nyuma nyuma,hesabu zake zilikuwa kali na alichukuwa bastola yake akaiweka kiunoni,akakanyaga mafuta mengi na kulipita gari la Mtui kisha kusimama mbele,akashuka na kumpungia mkono kana kwamba wanafahamiana.
Mtui alikuwa ndani ya gari,alimuona na kumuangalia kwa umakini zaidi jinsi mtu huyo anavyompungia mkono, ikamletea picha kuwa wanafahamiana lakini hakujuwa ni wapi walionana,akapunguza mwendo taratibu kabisa mpaka kumfikia Black Ninja miguuni,akashusha kioo.
“Bwana Deo Karekezi,habari yako?”
Kauli hiyo ilimfanya Mtui ashtuke kidogo lakini hakutaka kulionesha jambo hilo waziwazi.
“Nzuri tu,wewe nani?”
“Mimi mimi ni…”
Black Ninja hapohapo, akachomoa bastola yake kutoka kiunoni bila mtu yoyote yule wa pembeni kujua.
“Teremka ndani ya gari Deo sasa hivi kabla sijakuuwa,fanya haraka”
Kufumba na kufumbua alikuwa tayari yupo mateka,moyo wake ulipiga kwa kasi na jasho la kwapa lilianza kumtoka,isingekuwa suti aliyokuwa amevaa basi shati lake lingeonesha jinsi jasho lilivyojichora kwapani,kitu kilichomjia katika akili yake ni bastola yake iliyokuwa pembeni ya mlango, ilikuwa ni lazima aitumie tena kwa maarifa mengi sana.
“Shuka ndani ya gari”
Black Ninja alizidi kupiga mkwara.Kwa nje Black Ninja alidhani Mtui anafungua mlango wa gari kumbe alikuwa anasaka bastola yake iliyokuwa chini ya mlango,Zoezi hilo kwa Mtui lilitisha kwani maisha yake aliyafananisha na mchezo wa kamali kuuwa ama kuuliwa,ndiyo maana alitoa bastola yake kwa umakini,alivyohakikisha kaiweka vizuri mkononi,akashika kitasa cha mlango na kuufungua kwa nguvu.
“Paaa paaa paaaaa..Pyuu pyuuuu”
Zilikuwa ni kelele za bastola, risasi tatu zilifumuka kutoka ndani ya chemba ya bastola ya Mtui,zikazama ndani ya tumbo la Black Ninja,mbili zilitoka ndani ya bastola ya Black Ninja moja ilipiga kwenye kioo cha gari la Mtu ikapasua, hiyo ilimkosakosa lakini nyingine ilitua juu ya bega lake.
Balck Ninja alikuwa chini damu nyingi zinamvuja tumboni,akaanza kujiburuza akitambaa ili achukuwe bastola yake iliyokuwa kando,amfyatue Mtui.
“Paaaaaaa”
Mtui akaachia risasi nyingine ikapenya mgongoni mwa jambazi huyu gaidi aliyetumwa na Maximo kumuuwa Deo lakini siku hiyo kwake ilikuwa ni ya arobaini tayari,waendesha pikipiki waliokuwa kandokando walivyosikia mirindimo ya risasi waliacha pikipiki zao wakakimbia mpaka miguu yao ikagusa visogoni,wakina mama waliokuwa wanauza chapati asubuhi hiyo,walitoa mbio za ajabu kwani walikuwa wanajaribu kutetea roho zao!


Kufumba na kufumbua wafanyabiashara ndogondogo na waendesha pikipiki walitawanyika baada ya kusikia mirindimo ya risasi,hakuna mtu aliyekuwa tayari kupoteza maisha yake.Black Ninja, alikuwa chini damu zinamvuja anakoroma kama kondoo aliyechomwa kisu cha shingo hiyo ilikuwa wazi kwamba anajaribu kutetea uhai wake.Mtui alikuwa ameshika bastola yake ameegemea gari mkono wake mmoja unavuja damu nyingi sana, anamtizama Black Ninja aliyekuwa chini anajikunja kunja kama nyoka aliyemwagiwa mafuta ya taa, alikuwa makini akimtizama muuaji huyu huku akitafakari vitu vingi sana kichwani,dakika kumi baadaye ndipo Diffenda ya polisi ikafika eneo hilo.
Askari watano wakiwa na bastola mikononi mwao, walitua ardhini kwa uangalifu wa hali ya juu sana huku wakisogelea magari mawili ambapo pembeni alikuwa amesimama Mtui.Ni wazi kuwa baadhi ya raia walikimbilia kituo cha polisi kutoa taarifa za risasi hizo,ndiyo maana askari wakafika.
“Weka bastola chini mikono juu”
Askari mmoja akatoa amri kwa sauti akimwambia Mtui,mara moja akatii amri akatupa bastola yake chini na kuweka mikono yake hewani ili kusalimu amri,maaskari wengine wakasogea mpaka kwa Black Ninja aliyekuwa chini.
Taratibu zikafanyika hapohapo,Mtui na Black ninja wakapakiwa ndani ya Diffenda ili kupelekwa hospitalini kwa ajili ya matibabu kisha baadaye waongozane na maaskari kituo cha polisi ili kutoa maelezo.
“Huyu alifia njiani,risasi zilichimba ndani kabisa nyingine ilitokea upande wa pili mgongoni.Lakini vitu vyake hivi hapa huyu mwingine hali yake sio mbaya inabidi tuitoe risasi”
Dokta Lucas Kazimoto ndiye alitoa taarifa za kifo cha Black Ninja, akiwataarifu maaskari,ushahidi wa upande mmoja kwao ulikuwa tayari umefutika na ilikuwa ni lazima wamuhoji Mtui mambo yalivyokuwa alafu baadaye waanze kufanya uchunguzi wao wa kina.
Askari walikabidhiwa kila kitu cha Marehemu kuanzia simu,vitambulisho na mambo mengine.
“Ahsante sana daktari”
“Karibuni tena”
Maaskari waliondoka na kuingia moja kwa moja chumba alicholazwa Mtui,ambacho baada ya dakika kumi na tano baadaye alitakiwa kuingizwa ndani ya chumba kingine cha upasuaji ili risasi iliyokuwa ndani ya mkono wake itolewe mara moja kabla sumu haijaanza kusambaa kwenye damu.
“Naomba nimpigie mke wangu simu”
Mtui aliomba jambo hilo lifanyike kabla ya kuingia ndani ya chumba cha upasuaji,kuna roho ya umauti alihisi inamvamia kwani aliogopa sana kufa!
“Simu yako iko wapi?”
“Mfukoni,mfuko wa kushoto wa suruali”
“Sawa”
Nesi akaingiza mkono mfukoni mwa Mtui.
“Ingia kwenye majina tafuta jina WIFE,Kisha ipige alafu unipe”
“Sawa”
Tendo hilo likafanyika bila mahojiano mengine zaidi,Mke wa Mtui akapigiwa simu hapohapo,akawa kwenye laini na mumewe.
“Ndio Mke wangu…Nipo hospitalini…Niko salama..Nimepigwa risasi….ah ah ah sijaumia,nipo hapa Mwananyamala..Usilie sasa mke wangu,njoo Mwananyamala..Ndio naingia kwenye chumba cha operesheni nitakuhadithia,ni risasi ya mkono…Sawa sawa,tafuta dereva akuendeshe usiendeshe gari tafadhali..Ndio ndio”
Simu ilivyokatwa kiti alichokalia kilichokuwa na matairi chini, kilisukumizwa mpaka ndani ya chumba maalumu cha upasuaji ambacho kilimtisha kwani kilikuwa na mikasi mingi na taa kubwa mno,alihisi mwili wake unakufa ganzi hata kabla ya tendo hilo kufanyika,hiyo ilifanya mpaka jasho jembamba limtoke usoni,sababu katika maisha yake hakuwahi kuingia ndani ya chumba hicho kabla.
“Usiogope”
Dokta akamtoa wasiwasi!
*****
Deo Karekezi aliingia Tanga wilaya ya Lushoto saa tano na dakika thelathini na tano asubuhi,japokuwa alihisi uchovu lakini hakutaka kupumzika, alichotaka yeye ni kumuona Marietha wake na wala sio kitu kingine,pembeni yake kulikuwa na pikipiki nyingi sana zinazosubiri abiria wenye haraka kama yeye.Akasogea mpaka karibu kabisa!
“Shule ya Maduda,bei gani?”
“Hapo buku mbili N’goshii”
“Sawa twende”
Deo akakaa nyuma ya pikipiki,moyo wake ulikuwa unapiga kwa nguvu sio masihara na wakati mwingine alitamani afike mapema kwani alitamani kumuona Marietha wakati huohuo,aliamini kwa ushawishi mkubwa aliokuwa nao angeweza kumuimbisha na kumlainisha Marietha akakubali hata kama asingemkuta angewaomba ndugu zake wafanye hivyo.
Wakati dereva anaendesha pikipki yeye alikuwa katika msongo mkubwa wa mawazo na mpaka wanafika shule ya maduda aliendelea kuwaza tu!
“Zunguka kwa huku nyuma”
Baada ya kufika shule ya msingi Maduda pikipiki ikaingia mitaani,wakakunja kushoto na kunyoosha moja kwa moja.
“Mmmmh”
Deo aliguna ndani kwa ndani, kitu alichokiona kilimshtua na wakati mwingine alidhani amepotea kwani nyumba aliyokuwa anaishi Marietha zamani na Mama yake palikuwa na bangaloo yaani jumba kubwa la kifahari.Akageuka nyuma na kuangalia tena mazingira!
“Kaka hatufiki?”
“Subiri naona nimepotea,embu tuzunguke mtaa wa huku nyuma”
Pikipiki ikazungushwa na wakaingia mtaa wa nyuma lakini mazingira aliyoyakuta,bado hayakuendana kabisa na kumbukumbu zake za kichwani.
“Embu turudi tena kule”
“Kaka sikiliza,kwanza nipe pesha shangu.Naona unataka kunitapeli,nilipe kwanza pesha shangu”
Dereva wa pikipiki ambaye alikuwa ni Mgosi, alihisi kusumbuliwa sababu hayakuwa makubaliano yao kuzunguka namna hiyo na jinsi Deo alivyokuwa timtim nywele zake kichwani ilifanya imletee picha nyingine tofauti,hakuwa ana uhakika kama Deo ana uwezo hata wa kumiliki shilingi elfu kumi,sio siri alionekana kama kichaa wa barabarani.
“Unadhani sitokupa pesa yako?”
“Naomba shasha hivi”
“Bei gani kwani una nidai?”
“Shi elfu mbili bwana”
Deo akatoa noti ya shilingi elfu tano na kumkabidhi dereva.
“Embu turudi kule tulipotoka mara ya kwanza”
Deo na dereva wa pikipiki walizunguka eneo hilo karibia mara saba lakini jambo lilikuwa lile lile,kitu kilichomjia harakaharaka kichwani ni kuwa wenda eneo hilo liliuzwa na kununuliwa na tajiri akajenga nyumba yake.
Hata hivyo ilikuwa ni lazima aulize kwanza ni wapi watu waliokuwa wanaishi eneo hilo miaka iliyopita.Akashuka kutoka kwenye pikipiki na kuanza kutembea kwa mwendo wa kuchoka huku akitizama huku na kule,akalifikia geti na kuligonga,mapigo yake ya moyo yalikuwa bado yanapiga kwa kasi sana,akagonga tena geti kwa mara nyingine.Kwa mbali akaanza kusikia parakacha za mtu anatembea,akashusha pumzi nzito kidogo na kukaa sawa.
Geti likafunguliwa na mwanamke mnene kiasi maji ya kunde,kichwani amejitanda kitenge na mwilini kajifunga kitenge cha rangi hiyohiyo ya kijani,ilionekana kuwa ana pilika za kutoka siku hiyo.Akamtizama Deo kuanzia juu mpaka chini akawa kama anamfananisha, lakini bado hakuelewa kiumbe wa namna hiyo alimuona wapi.
“Mama Grace,shikamoo”
“Wewe nani?”
Kabla ya Mama Grace kuitika salamu, aliibuka na swali tena kwa ukali kidogo!
“Mimi Deo,Deo Karekezi.Mume wake na Marietha”
“Deo?Mume wa Marietha?Marietha gani?Nawewe Deo yupi?”
“Deo Karekezi”
Sio kwamba Mama huyu hakumjua Deo la hasha.
“Ndio Deo”
“Anyway,unataka nini?”
“Niruhusu kwanza niingie nina kiu sana Mama Grace,nilijua mmehama.Kidogo nipotee”
Bado Mama Grace aliendelea kumtizama Deo huyu aliyekuwa anaongea na kutoa harufu fulani mbaya,mbali na hapo hakutofautishwa na mtu anayetizama Kinyesi.Pesa za Tajiri Maximo zilifanya kazi kubwa na kubadilisha mpaka maisha ya ndugu zake wote kwa ujumla,hata wao hawakutaka tena kumsikia Deo katika masikio yao kwani walimuona kwa wakati huo hafai, ni sawa na nyoka wa kibisa mbaya zaidi walitamani abaki hukohuko gerezani, ndiyo maana hata Mama Grace alishindwa kuelewa imekuwaje Deo yupo uraiani wakati alihukumiwa kifungo cha miaka kumi na mitano, gerezani.
“Gerezani umetoka lini?”
“Juzi juzi tu hapa Mama Grace,sio siri maisha ya kule ni magumu sana.Kila siku niliomba Mungu nitoke ili nije kuwaona.Marietha yuko wapi?”
“Kwani hajakwambia alipo?”
“Sijaonana naye muda mrefu sana,nikaona nije hapa nimuulizie,naomba nimuone kama yupo ndani”
“Sikiliza Deo nikwambie,embu jiangalie kwanza ulivyo.Alafu tizama hii nyumba.Kwa harakaharaka nini umejifunza?”
Lilikuwa ni swali tata kidogo na Deo hakuweza kulifungua kiundani,ndio maana akabaki anajitizama na kuangalia nyumba hiyo kubwa iliyojengwa kisasa.
“Naomba nionane na Marietha”
“Huwezi kumuona na hautoweza kumuona kamwe”
“Kwanini?”
“Bwana wee,usiniulize maswali sina muda wa kujibu maswali hapa,kwanza ondoka Deo.Alafu kitu kingine fanya kama hujawahi kukutana na Marietha katika maisha yako na hapa usionekane tena”
Ilikuwa ni kama Misumari ya moto iliyotua juu ya kidonda kibichi,Deo alihisi kuumia moyo mno bado maneno ya Mama Grace hayakumuingia akilini,hakutaka kukubali kama ndiye huyu Mama ambaye kipindi cha miaka ya nyuma alikuwa anampa msaada wa kifedha.
“Mama Gr…”
“Toka hapa Deo,naomba nisikuone”
Hapohapo geti likafungwa,hakuna siku aliyohisi uchungu ndani ya mtima wake kama hiyo,alihisi kuchanganyikiwa na kuumia kwa wakati mmoja,alihisi kama amebeba dunia nzima kichwani,machozi yalimlenga na alihisi tayari mashavu yake yanalowana,alishindwa kujizuia na kujikuta analia machozi,akatembea mpaka pembeni na kuanza kulia kama mtoto mdogo.
Kila mtu aliyepita alimshangaa lakini yeye hakujali,aliamini ni kwanini anadharauliwa namna hiyo,alishajua ni kwanini anaonekana kama kinyago mbele za watu alijua kabisa ni kutokana na umaskini aliokuwa nao ghafla, ndiyo maana hata marafiki zake karibia wote aliokuwa anakunywa nao bia na kufanya nao starehe walipukutika kama majani mtini,hiyo ilimuuma zaidi na zaidi.
Aliendelea kukaa eneo hilo mpaka ilivyofika saa kumi na moja ya jioni,kuna Mwanamke mmoja alimuona huyu alimjua sana na aliamini atamsaidia ingawa hakuwa mwenye uhakika.
“Mama,Mama,Mama”
Mwanamke mfupi aliyebeba mkoba aligeuka nyuma baada ya kusikia anaitwa kwa muda mrefu,kabla ya kulifikia geti,akamtizama Deo.
“Mama shikamoo,Mimi Deo unanikumbuka?”
Mama huyu alimtizama Deo kwa kitambo kidogo, alionekana kama mtu anayevuta kumbukumbu kichwani.
“Mimi Deo Karekezi mume wake na Marietha”
“Mungu wangu Deo mwanangu!”
Mama alionekana kushtuka na kumuangalia Deo kwa masikitiko makubwa sana,siku zote katika maisha hata ukichukiwa na watu elfu moja, yupo tu mmoja kati ya hao atakuonea huruma,hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa mwanamke huyu aliyeitwa Vaileth,alimfahamu fika Deo kuanzia anaanza kumchumbia Marietha na matatizo yote aliyopitia.Alijisikia uchungu ajabu lakini hakuwa ana uwezo wa kubadili mambo yaliyokuwa yametokea,alichomsaidia Deo ni kumpa moyo na matumaini.
“Deo wewe ni mwanaume inabidi umalize swala hili kiume,usilie”
“Ma..ma inaumaaa…Nau..mia sana”
Deo alishindwa kujikaza,machozi yalimbubujika kama maji, yakalowanisha mashavu na kuchuluzika mpaka shingoni,hakuona aibu kulia mbele ya Vaileth ingawa kwa mwanaume kufanya hivyo ilikuwa ni mwiko.
“Usilie Deo,usilie nakuomba nyamaza.Pambana kiume.Mimi nitakuelekeza Marietha anapoishi mkayamalize.Sawa Mwanangu?”
“Sawa Ma…ma”
Deo alijifuta machozi akitumia viganja vyake vya mikono, alihisi kupata nguvu mpya kutoka kwa Mwanamke huyu Mkarimu ambaye kwake alimfananisha na Malaika siku hiyo,alivyoelekezwa hakuwa tena na sababu ya kusubiri,akapanda pikipiki kwani alitaka awahi kufika mapema, akaonane na Marietha wake,alitafakari na kichwani alijiuliza maswali mengi sana.
“Broo,kumbe ulikuwa unafika hapa?”
Dereva wa bodaboda alimuuliza abiria wake baada ya kumfikisha nje ya jumba kubwa lenye gorofa tatu, ambalo lilimfanya Deo ashangae pia.
“Ndio kaka”
“Huyu Mama anayeishi hapa ni ndugu yako?”
“Mama yupi?”
“Si huyu awara wa Maximo”
“Maximoo?Maximo gani?”
“Kaka humjui Maximo kwani?Mzee mmoja ana pesa chafu,tunamwita Tycoon kwani wewe sio mwenyeji wa huku?”
“Hapana”
“Wakubwa wanafaidi bwana”
Dereva wa pikipiki,alipiga soga huku akitafuta chenji ndani ya mfuko wa shati lake,akamkabidhi Deo na kuondoka zake.
“Ndio hapa kweli?Ni hapa lakini,nguzo na matofali yale pale.Ndio hapa”
Deo alijaribu kufananisha maelekezo aliyopewa na Vaileth na eneo alilokuwepo.
“Marietha anafanya kazi humu au?”
Maswali ambayo hayakuwa na majibu, yalizidi kumiminika ndani ya kichwa chake huku akitembea kuelekea kwenye geti kubwa,akabonyeza kengele.
“Ding dung”
“Ding Dung”
Kengele ikasikika tena,Deo akasikia kama kuna mtu anatembea.Geti likafunguliwa!
“Habari yako”
Mlinzi ndiye aliyetoa salamu,Deo akarudisha majibu.
“Nikusaidie nini?”Mlinzi akauliza kwani ulikuwa wajibu wake.
“Kuna mwanamke namuulizia, anaitwa Marietha,sijui ndio hapa?”
“Ndio hapa”
“Yupo?”
“Ndio yupo”
“Naweza nikamuona?”
“Subiri kidogo”
Mlinzi alifuata miiko ya kazi yake,ilibidi kabla ya kufungua geti aingie ndani kwanza akaombe Ruksa kwa tajiri yake, ndio taratibu nyingine zifuate.
Maisha ya Marietha kwa kifupi yalikuwa kama paradiso ama peponi sababu yalikuwa ya raha mustarehe,shida kwake zilimpita kando, chochote alichokuwa anahitaji kilifanyiwa kazi na Maximo ndani ya muda mchache,kwa maana hiyo alipanda bei na alijihisi alitoboa kimaisha, yeye ndiye yeye duniani.
“Hodi Mama”
Siku hiyo akiwa seblen amejiachia kwenye makochi miguu juu na kimini chake,alisikia sauti kutoka kwa mlinzi,akasimama na kutembea mpaka dirishani,akafungua pazia.
“Kuna nini tena Pascal?”
“Kuna mgeni wako nje”
“Nani?”
“Hajanitajia jina lakini anasema ana shida nawewe”
“Mwambie apite lakini si nilikwambia uwe unawauliza kwanza majina”
“Ndio Mama, samahani nimesahau”
“Mfungulie apite”
Marietha akarudi juu ya kochi na kujitupa,kuna tamthilia ilikuwa imemteka kwa kiasi cha kutosha,ndio maana hakutilia maanani sana ni aina gani ya mgeni anataka kuzungumza naye jioni hiyo.
“Ngo! Ngoo! Ngooo!”
Mlango ulisikika ukigongwa.
“Karibu”
Marietha bila kugeuka nyuma alisema,mlango ukafunguliwa.Hapo ndipo alipogeuza shingo yake nyuma ili ajuwe ni mgeni wa aina gani anaingia ndani kwake.
Moyo wa Marietha ulikita kwa nguvu sana,mtu aliyesimama mbele ya macho yake, hakuelewa kama alimtisha ama alimuogopesha!Sababu alihisi hali ya utofauti mwilini.
“Mariethaaaa!”
Deo aliita kwa sauti ya chini huku mapigo yake ya moyo yakiwa yanadunda,akahisi kama uti wake wa mgongo umepigwa na ubaridi,butwaa alilopigwa halikuwa na kipimo chake!



Hakuna kipingamizi kutoka kwa watu wa mwambao waliosema kwamba ‘Maskini akipata matako hulia mbwataaa!’na semi zao siku zote zinakuwa na ukweli ndani yake kwani Deo Karekezi aliliamini hilo asilimia zote mia moja,Marietha alimbadilikia na kumuangalia kama mtu anayetizama matapishi ya mlevi,hakuwa Marietha wa nyuma ambaye alikuwa myenyekevu na msikivu siku zote.
Pesa za Maximo zilimbadilisha, akamvimbia Deo na kudiriki kumwambia kuwa aondoke tena ananuka kama beberu la shamba,Marietha alitamka maneno mazito na matusi ya waziwazi, hilo lilimfanya Deo aumie zaidi na zaidi.
“Ulinitesa sana Deo.Mungu ni mkubwa ana jaribu kukuonesha kitu,tizama ulivyomnyanyasa Issa kipindi kile,kwanini nilikupenda sijui?Deo siwezi kuwa nawewe,nenda tu”
Marietha alizidi kutoa kauli hizo.
“Kitu kingine,embu jitazame ulivyo niangalie namimi nilivyo.Unahisi tunaendana?Hatuendani kabisa na siku zote ndege wanaofanana ndio huruka pamoja,huwezi kumkuta kunguru kwenye kundi la njiwa”
Marietha alizidi kuongea kwa kiburi huku akibenua mdomo wake,hiyo ilifanya Deo azidi kushangaa,moyo ulimuuma kupita kiasi.Hakuamini kama Marietha huyu ndiye anamchambua na kumchamba kwa kejeli namna hiyo,alitamani kumvaa kwa hasira lakini aliogopa kurudi tena gerezani.
“Marietha naomba unisamehee mke wangu najua hizi mali ndio zinakusumbua lakini kwanini tusirudiane,bado nina uwezo wa kuzitafuta na kurudi kama zamani”
“Deo,sitaki uniimbie nyimbo zako.Naomba nikukumbushe kitu,mwenyewe akikukuta humu ndani.Hautopenda,naomba uwende kama unapenda kuishi”
“Marietha mke wangu…”
“Mimi sio mkeo,Mimi sio mkeo unikome.Unikome kabisa”
“Nipo chini ya miguu yako,rudi nyumbani tulee watoto mke wangu”
“Ha! Haaa! Haaaa!Deo una nyumba gani wewe?”
“Ninaishi na Mtui lakini tutaondoka pale.Tuanze maisha yetu”
Deo aliporomoka mpaka chini na kupiga magoti,akatembea mpaka kwenye miguu ya Marietha huku akimwaga machozi na kuomba msamahaa lakini hiyo ilikuwa ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa acheze mziki.
“Deo,nilikupenda sana lakini mimi nawewe naomba ibaki historia tu”
“Kis…a hii nyumba na hayo magarii ha..po nje?”
“Kisa nimeamua kuanza maisha yangu upya.Na naomba uwende”
“Wato..to wako wapi?”
“Wewe wa nini?”
“Naomb..a niende nao”
“Sahau”
“Naomba niwao..ne”
“Huwezi kuwaona,ili iweje? Deo nenda tafadhali.Ondoka Deo”
“Mari..etha”
Hata kama angelia machozi ya damu,isingekuwa rahisi kubadili akili ya Marietha ambaye tayari alikuwa anaishi maisha ya kitasha,kwanini aende kwa Deo tena kwa mfano?Wakati alikuwa anaishi kama Malaika, haikuwezekana tena sababu Deo alikuwa dume suruali,hana tena thamani kwake.
“Deo toka”
Marietha akazidi kusisitiza,akamuinua Deo na kuanza kumsukumiza.
“Sawa,nahitaji kuona watoto”
“Nishakwambia huwezi kuwaona nenda basi Deo”
“Siwezi bila kuwaona”
Nisubiri hapo uwaone,Marietha alisema huku akitoka nje na alivyorudi ndani alikuwa na mlinzi pembeni yake.
“Sitaki kumuona huyu kiumbe hapa ndani,mtoe nje na asiingie tena humu ndani”
Mlinzi wa getini ambaye alitoka katika kampuni ya SK Security alipokea maagizo hayo na kufanya kazi yake dakika hiyohiyo,alimvuta Deo na kuanza kutoka naye nje.
“Mariethaa,Mari…”
“Kaka,toka nje.Tusiharibiane kazi basi”
“Huyu ni mke wangu”
“Namimi ni tajiri yangu.Toka nje”
Jinsi Deo alivyovutwa haikuwa picha nzuri hata kidogo,kilikuwa ni kitendo cha udhalilishwaji kwa kiasi cha kutosha,alitolewa nje na geti likafungwa na kufuli.
“Asiingie tena humu ndani”
Huyu ndiye Marietha ambaye kufumba na kufumbua alikuwa ana amrisha kama Rais wa nchi fulani,pesa za Maximo zilimtia kiwewe na zikamvimbisha kichwa!Marietha hakuwa na huruma tena,kurudiana na Deo kulimaanisha kurudi kwenye shida ambazo alikuwa tayari amepishana nazo kando.Usiku wa Saa mbili alipokea simu kutoka kwa Maximo akimwambia kuwa yupo Dar es salaam kibiashara.
“Utarudi lini baby?Mbona ghafla?”
“Kesho kutwa,ni biashara ndogo tu namalizia”
“Sawa baby take care”
“Ahsante”
Maximo alivyokata simu aliiweka mezani na kumtizama Kamanda Arafa Likungwa,kamishna wa jeshi la polisi, wilaya ya Temeke.Kuna mambo walikuwa wanajadili kuhusu kijana wake wa kazi Black Ninja, na niya ya kumuita Kamanda huyu New African hotel, ilikuwa apate naye faragha.
“Naona tusiongee sana huyu ni kijana wangu.Mimi sipendi kusumbuliwa,embu futa hilo faili na ulichome moto”
“Mambo haya hayaendi kienyeji Mzee.Kuna taratibu zake, inabidi niongee na wakubwa wangu wa kazi.Hawatonielewa”
Maximo alielewa nini maana ya sentensi hiyo kutoka kwa Kamanda Arafa Likungwa,ilikuwa ni lazima atoe kitu kidogo kwani penye uzia ilikuwa ni lazima upenyeze rupia.
“Kamata milioni tano hii choma hilo faili moto,hii milioni saba nyingine utanunua mboga usiku,ule na familia yako”
Mzee Maximo alitoa baasha mbili za kaki, ilionekana pesa hizo alizitenga kabisa kwa ajili ya kazi hiyo,zilikuwa ni pesa nyingi sana kwa Afande huyu ndiyo maana alianza kujichekesha.
“Sasa hapa inabidi nikaongee na Mwita ili afute hiyo kesi,kazi imekwisha Mzee.Chukua namba zangu,ukipata shida yoyote ile nipigie simu.Mimi ndio mkuu wa askari wote wilaya hii ya Temeke”
Maneno yalimtoka Afande na walibadilishana namba,faili la Black Ninja na kesi ya kuvamiwa kwa Mtui vikafutwa na kesi hiyo kuanzia siku hiyo haikuendelea tena, kila askari alizibwa mdomo na pesa za Maximo,zoezi hilo lilivyokamilika baada ya siku tatu, Maximo aliingia ndani ya gari na kuondoka na msafara wake kwa safari ya kurudi mkoani Tanga!

*********
Siku zote ukitaka kuheshimika duniani ni lazima uwe na pesa hata kama ukiwa mtoto mdogo, utapewa shikamoo na wazee,hayo ndiyo yalikuwa maisha ya Deo miaka michache iliyopita.Lakini leo hii kwake mambo yalikuwa kinyume chake,alidharauliwa kila alipopita.Hakupewa tena heshima kama kipindi cha nyuma alivyokuwa ana badilisha magari kama nguo,kipindi hiko ana marafiki wengi,kila anapokaa ni lazima atazungukwa na watu,alimuwaza rafiki yake mkubwa aliyeitwa Ayambo.Ambaye siku zote kwenye starehe, walikuwa pamoja,akamkumbuka binamu yake aliyeitwa Hillary Tilihongerwa, meneja wa Cement katika kiwanda cha Dangote,hakumsahau Bright Kimaro meneja manunuzi katika kampuni ya TBL.
Moyo ulimuuma alivyokumbuka starehe alizokuwa anafanya,alitamani mambo yanayotokea yawe ndoto ashtuke lakini haikuwa hivyo kwani ilikuwa ni halisi kabisa.
“Eh Mungu”
Alisema Deo akiwa ndani ya basi anatafakari maisha yake yalivyokuwa yanaenda kiujumla, wakati mwingine alitamani kujinyonga ili afe,kila alichokuwa nacho kilipotea,kifupi tayari alikuwa maskini asiye na mbele wala nyuma.Hakutaka kuendelea kubaki mkoani Tanga kwani angezidi kuumia, mbali na hapo hakuwa na ndugu ama rafiki hata mmoja,ndiyo maana siku iliyofuata aliamua kuchukua maamuzi ya kurudi jijini Dar es salaam,akafikie nyumbani kwa Mtui.
Kitendo cha kufika Ubungo saa sita mchana, alitafuta daladala ambayo ilimpeleka mpaka Tegeta.Alivyowasili aligonga na kufunguliwa geti na mlinzi wa kimasai.Akanyoosha mpaka seblen,kuna kitu kilimshtua sana!Mtui alikuwa amelala seblen kwenye kochi,mkono wake una bandeji kubwa mno.
“Mtui”
Akaita,kwa Mbali Mtui alisikia na kufumbua macho yake,alivyogundua ni Deo akakaa sawa.Hapo hakuweza kukaa kimnya,ilibidi aulize nini kilimsibu rafiki yake.
“Nilipigwa risasi,nilivamiwa”
Mtui alifunguka na kusema mkasa wote ulivyotokea mpaka akapigwa risasi ya bega!
“Alafu nilishangaa huyo mtu alikuwa anataja jina lako”
Mtui alisema baada ya kumaliza mkasa mzima mpaka akavamiwa na kupigwa risasi!
“Ulisema alitaja jina langu. Kivipi?”
“Alivyotoa bastola aliniambia Deo shuka,hata alivyonisalimia pia”
Deo alitafakari kidogo lakini bado hakuweza kufafanua vizuri nini maana yake sababu alikuwa mwenye ‘stress’ nyingi sana katika kichwa chake.
“Pole sana Mtui”
“Ahsante”
“Polisi wamesemaje?”
“Huyo jambazi,niliyempiga risasi alifia njiani.Wakachunguza na kutaka kibali cha bastola yangu nikawaonesha,leo nimeenda wananizungusha huku na kule.Nikaachana nao,vipi huko?Ulimuona Marietha?”
Deo akaulizwa swali lililomfanya anyong’onyee,hakuwa na sababu ya kuweka mambo ndani ya kifua chake,akasema kila kitu, mpaka alivyotimuliwa na Marietha.
“Pole sana,ndio maisha yalivyo Deo!Jikaze kiume, nenda kaoge ukapumzike mimi mkono bado unaniuma,kesho naenda kufanya tena dressing”
Kazi ya kumuuguza Mtui kuanzia siku hiyo aliivaa Deo na Mke wa Mtui na walimuhudumia siku nne mfululizo,walimpeleka hospitali na kumrudisha.
***********

Hakuna siku iliyomtibua Mzee huyu Maximo baada ya kuingia ndani ya chumba cha Kamera za CCTV na kumuona Mwanaume aliyemtambua kwa jina la Deo Karekezi, ambaye alitakiwa afe,mbaya zaidi alihitaji watoto jambo lililomfanya atibuke kama Kiboko mtoni,hasira na wivu vilimpanda kwa wakati mmoja.Hapohapo, akainua mkonga wa simu.
“Kishoka”
“Naam Mkuu”
“Unaijua shule ya St.John?”
“Sekondari au Primary?”
“Primary”
“Ndio”
“Kuna watoto wanasoma pale.Mmoja anaitwa Abraham na William,nenda kawachukuwe.Wapo darasa la tano”
“Alafu?”
Hapo Maximo alikaa kimnya kidogo,kuna kitu alikuwa anakifikiria.
“Fanya unavyojua, wasionekane kwenye uso wa dunia”
“Una maana gani bosi?”
“Kill them”(Wauwe)
“Sawa”
“Ukimaliza hilo nitakupa kazi nyingine,utaendelea alipoishia Black Ninja”
“Okay”
Maximo alikata simu na kuyabana meno yake kwa hasira,aliamini kivyovyote vile Abraham na Wiliam ndiyo wanawaunganisha Deo na Marietha,alitaka kuwauwa ili akate waya!Kisha baadaye ammalize Deo Karekezi,huo ndio ulikuwa mpango wake,ilikuwa ni lazima asonge mbele hata kama Black Ninja hayupo.Maximo alikuwa ana sura mbili,Malaika na Shetani.
Mambo yalipangwa na kwenda kama ilivyotakiwa kwani siku hiyo Marietha aliwasubiri watoto wake mpaka usiku bila kuwaona,wasiwasi ulimuingia na kumpigia dereva simu,jibu alilopewa lilifanya mapigo yake ya moyo yabadili mwendo.
“Hawapo..Nani kawachukuwa?Mungu wangu…Sawa nakuja”
Marietha aliwasha gari usiku huohuo mpaka shule ya St.John,moja kwa moja aliingia ofisini ili kujua watoto wake walipo.
“Kuna Mwanaume alikuja hapa,mrefu mweupe kasema ni mjomba wao.Akawachukuwa”
Mwalimu Diana alisema na kuelezea jinsi mwanaume huyo alivyofanana,hakukua na haja ya kuuliza kitu kingine zaidi.
“Deoooo!”
Marietha aliropoka na akili yake ilimtuma moja kwa moja ni lazima atakuwa Deo amehusika na tukio hilo,ambalo kwake alilifananisha na utekaji.
“Deo lazima nikufunze adabu,nilikwambia uachane na wanangu naona husikii.Lazima urudi tena gerezani”
Marietha aliongea huku akiendesha gari kurudi nyumbani kwake,ilikuwa ni lazima amzukie Deo Dar es salaam mapema kukikucha, ndiyo maana baada ya kufika nyumbani kwake akampigia simu dereva anayemuendeshaga akimwambia kwamba ajiandae asubuhi na mapema kuna safari.
“Kesho asubuhi sana Masudi”
“Sawa Mama nitakuja,ni safari ya wapi?”
“Dar es salaam”
“Saa kumi na moja nitakuwa hapo”
“Usichelewe”
“Sawa Mama”
Roho ya chuki na hasira zilimvaa Marietha ghafla,alichukia ajabu na alitaka kumfunza Deo adabu na kumuonesha kuwa ana uwezo wa kumfanya chochote kile na asimchezee akili.
“Asinichezee akili yangu, asipoangalia atarudi gerezani mbwa yule”
Marietha aliongea huku akiwa kitandani anatafakari na kutamani kukuche.
***********

Ratiba ya Deo ilijulikana ingawa hakuwa ana kibarua chochote,asubuhi aliwasha gari na kumpeleka Mtui hospitalini kisha kumpitisha ofisini kwake na jioni kumpitia.Mtui hakuweza kuendesha gari na Deo ndiye aliyekuwa anamsaidia mambo mengi na shughuli za hapa na pale huku mkewe akihakikisha Mtui anakula na kulala vizuri,siku hiyo kama kawaida Deo aliamka na wote wakawa mezani wanapata kifungua kinywa.
Ghafla walisikia geti la nje linabamizwa kwa nguvu, ilielekea kuna mtu aliingia na kulifunga kwa hasira.Wote wakashtuka,sekunde moja baadaye mlango wa seblen ukafunguliwa kwa nguvu pia.
“Deo watoto wangu wako wapi?”
Bila Salamu Marietha aliuliza kwa ghadhabu,hilo lilifanya kila mtu apigwe na butwaa.
“Deo usiniangalie,watoto wangu wako wapi?”
“Watoto gani?”
Deo akajibu kwa swali lakini jambo hilo Marietha alilitafsiri kama maigizo!
“Usiniletee maigizo Deo,nipe watoto wangu”
“Marietha mbona sikuelewi”
“Hujawahi kuuona upande wangu wa pili,subiri nikuoneshe”
Marietha aliongea huku akiingiza mkono wake ndani ya mkoba wake,akatoa simu yake na kubonyeza bonyeza kisha kuiweka sikioni.
“Yes baby…Ndio nilikuaga asubuhi nakuja Dar,Yule mtekaji watoto nishamuona sasa analeta ubishi,okay baby ongea nao,wapigie…Sawa....Mimi nipo hapa nasubiri..Tegeta Nyuki nyumba namba 18 waambie waje hapa”
Hapohapo Marietha alikata simu na kumtizama Deo,Mtui pamoja na Mke wa Mtui.
Hawakuelewa ameongea na nani lakini walijuwa aliongea na mwanaume ambaye kivyovyote vile alikuwa ana mahusiano naye.Dakika tisa baadaye walisikia geti linagongwa,lilivyofunguliwa waliingia askari kumi na mbili,wakiwa na mitutu wengine wameshika virungu mikononi.
“Askari Mimi ndio Marietha”
Marietha alijitambulisha.
“Hiro rijambarika riko wapi?”
Aliuliza Afande Chacha,kwa rafudhi ya kikurya na alionekana kuwa mwenye kiherehere kuliko askari wengine wote.
“Yule pale”
Afande Chacha, akamsogelea Deo na kumtandika kibao cha uso.
“Haroo twende huku”
“Marietha kwanini unafanya hivi?”
Mtui aliingilia, alivyoona hali ishakuwa mbaya.
“Mtui nyamaza,mnafki mkubwa wewe.NAKUCHUKIA SANA”
Mke wa Mtui alivyodakia nayeye alitulizwa na matusi.
“Nawewe ndiyo nyamaza kabisa,sijui nikuweke kwenye kundi gani.Malaya mkubwaaa”
Marietha aliibua sekeseke,Deo akachukuliwa na kutolewa nje kama jambazi,kilikuwa ni kitendo cha kinyama mno!
“Afande sikilizeni,kirungu kimoja elfu tano! Viwili elfu kumi”
Marietha alitoa kauli,ikawa kama Mbwa wenye njaa kali wamefunguliwa bandani kwani Deo alipigwa virungu visivyokuwa na idadi kamili,vikampasua mwili mzima.Damu nyingi zilimtoka usoni na mdomoni,mbali na kuomba msamahaa lakini waliendelea kumshambulia,mwisho walimpasua vibaya sana.Uso wa Deo,haukutambulika tena na mdomo wake ulikuwa tayari umechanika kama kipande cha gazeti.



Hakuna mtu aliyekuwa tayari kuamini tukio linalotokea mbele ya macho yao,Marietha kufanya jambo hilo la kinyama tena kwa mumewe wa Ndoa ambaye walikula kiapo kanisani watapendana mpaka mmoja wao atakaporudi mavumbini.
Ilikuwa ni asubuhi na mapema lakini majirani walifungua milango yao na kuangalia tukio hilo la polisi kumpiga mtu kama mwizi.
“Yule ni mwizi au?”
Mzee mmoja aliyekuwa amevaa taulo alimuuliza mwenzake baada ya kufungua mlango,jinsi Deo alivyokuwa anashambuliwa na askari ilikuwa picha tosha ya swali hilo.
“Mimi sijui,wametoka naye ndani kwa Mtui”
“Au ndio walitaka kumvamia tena?”
“Inawezekana”
Majirani walisemezana lakini hakuna hata mmoja wao aliyeweza kukitegua kitendawili cha mtu huyo anayepigwa.Deo aliburuzwa mpaka karibu na Difenda huku akimiminiwa mvua ya virungu,kufumba na kufumbua hakutamanika, uso wake ukawa kama nyama ya ng’ombe buchani,amepasuka pasuka, damu zinamchuluzika.Mtui na mke wake walikuwa nje na walishuhudia kitendo hiko lakini hawakuwa na la kufanya kwani askari hao walikula pesa nyingi, waliendelea kufanya kazi yao,wakampandisha Deo juu ya Diffenda na kumtupa,askari mmoja akapanda juu na kumsindikiza na mguu wa shingo.
“Dulla,twende”
Dereva ambaye nayeye alikuwa ni askari, akapiga gari moto na Diffenda ikazunguka kwa kasi na kuondoka zake,Marietha akaingia ndani ya gari ya gharama aina ya BMW X6, ambapo ndani kulikuwa na dereva tayari.
“Hapana,Washa gari nasisi twende”
Mtui akamwambia mkewe,wakarudi ndani na wao wakaanza safari ya kufukuzia Diffenda kwa nyuma,lilikuwa ni jambo la kuuzunisha, ilikuwa ni lazima wajuwe Deo kafanya kosa gani na kwanini kapigwa namna ile.
Marietha alishageuka tayari na kuwa shetani,hakutaka kumsikiliza mtu yoyote, isipokuwa watoto wake wapatikane.
“Lazima nimfunze adabu”
Marietha alisema akiwa ndani ya gari,mbele yake aliliona Diffenda ya polisi yeye alikuwa nyuma yao.
“Diffenda isikupotee hiyo”
Akamwambia dereva wake.
“Sawa Mama”
Dakika ishirini baadaye walikuwa Kituo kikubwa cha polisi Urafiki,Deo akateremshwa.Bila kuchukuliwa maelezo yake akatupwa nyuma ya nondo.
“Enhee Mama jambazi ndio huyu?Una uhakika ana watoto wako?”
Askari aliyekuwa mapokezi alimuuliza Marietha akiwa ameshika kalamu na karatasi.
“Ndio nina uhakika”
“Unaishi wapi?”
“Tanga”
“Kwahiyo watoto aliwateka vipi?”
“Watoto wangu wanasoma shule,alimtuma mtu aende kuwachukuwa”
“Nini kinakufanya mpaka uhisi kama yeye ndiye kawachukuwa wanao?”
“Alikuja Tanga akaniambia anawataka watoto”
“Ana wataka watoto, kivipi?Una uhusiano naye gani?”
“Alikuwa mme wangu”
“Alikuwa Mme wako?Kwani mliachana?”
“Ndio”
“Nipe separate sheet”
“Separate sheet ndio nini?”
“Barua ya mahakamani inayoonesha kuwa mmetengana”
“Hiyo sina”
“Hao watoto huyo ni baba yao?”
“Ndio.Hapana, mmoja ndio mtoto wake”
“Sasa kwanini msingemalizana hukohuko kuliko kuja hapa polisi?Unajua maana yake?”
Afande Lukundo alimuogesha Marietha mvua ya maswali kabla ya yote,alielewa kwa kesi kama hiyo haikupaswa wanandoa hao kufika hapo lakini kutokana na amri aliyopewa na mkubwa wake wa kazi hakuwa na jinsi ingawa alijuwa anaenda kinyume na sheria.
Sasa angefanya nini?Wakati mkubwa kasema, ilikuwa ni lazima afuate amri ya mkuu wake wa kazi.Dakika moja baadaye Mtui aliibuka akiwa na mkewe kushoto,moja kwa moja mpaka kaunta kwa askari.
“Habari yako afande”
Akatoa salamu.
“Nzuri,una shida gani?Na huo mkono vipi?”
“Nilipata ajali”
“Shida yako?”
“Kuna ndugu yangu ameletwa hapa sasa hivi na Diffenda”
“Kwahiyo unatakaje?”
“Nataka kumdhamini”
“Jina lake nani?”
“Deo Karekezi”
Afande Lukundo akaachana na Marietha akaenda mpaka kwenye nondo.
“Deo Karekezi,Deo Karekezi”
Akaita,Kwa mbali Deo alisikia akiitwa lakini hakuweza hata kujigusa kwani aliumia vibaya sana.Kwa nguvu akajikokota na kuitikia.
“Haa!kumbe ndio wewe.Subiri hapo wewe mtekaji”
Afande Lukundo akarudi mpaka Kaunta na kumueleza Mtui kosa la Deo Karekezi.
“Hapana afande sio kweli”
“Huyo Mama pembeni ndio kamleta hapa”
Afande akasonta kidole kwa Marietha,wote wakageuka.Kwa dharau na nyodo akajifanya kama hajawaona na kugeukia upande wa pili.Mtui akajitosa na kumsogelea karibu.
“Marietha,kwanini unamfanyia hivi mumeo wa ndoa?”
Badala ya Marietha kujibu alitingisha mguu huku akimpandisha Mtui kuanzia juu mpaka chini,Mtui alitafsiri kitendo hiko kama dharau lakini hakujali.Ilikuwa ni lazima ashuke ili Deo awe huru.
“Marietha,nini tatizo?”
Mtui akauliza kwa upole na unyenyekevu wa hali ya juu.
“Kwani wewe hujui?”
“Kama ningekuwa najua nisingekuuliza”
“Unajua sana,Unajua sana Mtui.Nawewe usipoangalia utamfuata mwenzako”
“Kuna nini lakini?Deo amefanya nini?”
“Watoto wangu wako wapi?”
“Watoto wako?Mbona sikuelewi”
“Huna hata aibu,najua hii njama aliyofanya Deo nawewe amekwambia ni lazima.Sasa atakula jeuri yake,yeye si kamwaga ugali mimi nimemwaga mboga na maji ya kunawa,hali mtu”
Marietha alisema na kusukumia kauli yake na misemo ya kiswazi ili tu aonekane anamaanisha.
Hata yeye alijishangaa roho hiyo ameitoa wapi.
“Marietha,watoto gani ambao unazungumzia wewe?Abraham na William,au wengine?”
“Alafu tuzivunjiane heshima,unadhani nina watoto wangapi”
“Nimeuliza tu”
“Ndio hao Deo kawachukuwa”
“Sio kweli”
“Wewe na Deo hamna tofauti yoyote ile sasa nataka niwaoneshe”
Huo ndio ulikuwa msimamo wa Mwanamke huyu Marietha.
**** ****
Mguu mmoja wa Katrina ulikuwa begani kwa Issa na mwingie umekunjwa vizuri yupo juu ya kitanda,Issa yupo juu yake, anazungusha kiuno chake wanafanya mapenzi!Tayari walikuwa wameshatoka kupasha kwa kupigana madenda na kushikana shikana kila sehemu za miili yao,kila mtu siku zote alimuona Mwenzake mpya na hata siku moja hawakuchokana.Katrina na Issa walikuwa na mapenzi ya dhati na walikuwa ni miongoni mwa familia zilizopiga hatua katika mafanikio.Katrina alikuwa ni mwanamke mchapakazi na kila siku alifikiria kufungua vitega uchumi,hakubweteka ingawa wakati mwingine Issa alimuangusha hiyo haikumvunja moyo, aliendelea kupambana kama mwanajeshi vitani na silaha yake siku zote ilikuwa ni akili aliyopewa na Mungu!Alimpenda Issa kwa moyo wake wote sababu walipitia vitu vingi sana huko nyuma,ndiyo maana kila siku alimuona mpya,utamu aliokuwa anausikia baada ya ndizi ya Issa kuwa ndani ya mgodi wake haukuweza kuelezeka.Issa alijitahidi kumridhisha mkewe ndiyo maana kila dakika alibadilisha mkao,akamuweka vizuri kwenye kona ya kitanda na kurudisha ndizi yake ndani ambapo alizidi kumsugua.
“Aaaah aaaah aaaah aashss aaah Iss..a aaah yeees yeees aaah aaaaah”
Hizo ndizo kelele alizokuwa anatoa Katrina huku akimfinyia Issa kwa ndani,baada ya sekunde tano akabinuliwa na kuwekwa Kifo cha Mende,Ndizi ya Issa ilikuwa ndani na walikuwa wananyonyana ndimi kwa fujo, ilielekea kila mtu alikuwa anakaribia kufika kitonga,Ndiyo maana Katrina alianza kuukwaruza mgongo wa Issa huku akilalamika na kutoa miguno,hiyo ilifanya mpaka ngozi yake ya mwili ibadilike rangi,Issa akazidisha kasi na mwishowe akapasua yai la bata,akamlalia Katrina kifuani huku gari yake ikiwa bado ndani ya maegesho.
“I love You Issa”(Nakupenda Issa)
Katrina alinong’ona kwa kudeka akiwa chini ya Issa,akamvuta mdomo na kumpa ulimi wakaanza kunyonyana tena midomo.
“Nakupenda pia”
“Nataka tuongeze mtoto mwingine”
“Lini?”
“Nitakwambia,nataka tuzae mwingine”
“Sawa mke wangu”
Kilichomtoa Issa kutoka Kitandani ni baada ya simu yake kuita,umbali kutoka kitandani na meza ilipo ulikuwa ni mrefu kiasi kwani chumba kilikuwa kikubwa sana.Akatembea mpaka mezani na kupokea simu.
“Vipi Misango?Umefikia wapi?”
Issa aliongea kwa sauti ya chini ilionekana kuna jambo la magendo alilotaka kumficha Katrina!
“Bado tunamsaka,majuzi nilisikia ameenda Tanga lakini leo nikasikia tetesi kuwa yupo kituo cha polisi hapa Dar”
“Kituo cha polisi?”
“Ndio amekamatwa”
“Na nani?”
“Sijui lakini ameshikiliwa”
“Kituo gani?”
“Urafiki”
“Sasa itakuwaje?Mimi namtaka huyo kiumbe,nataka nimfanye kitu kibaya ambacho hatosahau katika maisha yake”
“Tusubiri atoke, au?”
“Sawa,utanijulisha kilichotokea.Utanipa feedback”
Simu ilivyokatwa Issa akabadili mazungumzo na kujifanya bado yupo kwenye laini, anaongea kuhusu biashara na mteja,tena aliongeza sauti ili kumpumbaza mkewe asielewe.
“Ndio ndio,Kesho bwana leo Jumamosi si unajua nipo Off na familia kidogo.Okay Jumatatu Shekh wangu.Msalimie Abdulkarim.Insha Allah Insh Allah”
Issa alimaliza kuzuga lakini kichwani ilikuwa ni lazima amteke nyara Deo Karekezi ili amfunze adabu,bado kitendo cha udhalilishwaji alichomfanyia miaka ya nyuma iliyopita, kililimbikiza chuki na kujenga kisasi!
*******
Gari aina ya Nissan Patrol ilikuwa katika mwendo wa kasi ya ajabu na iliendeshwa na bwana Kishoka,pembeni ya gia kulikuwa na bastola iliyofungwa kiwamba cha kutoa sauti.Mguu wake ulinyooka kumaanisha kwamba gari ipo katika mwendo wa kasi.Kazi aliyokuwa ametumwa na Mzee Maximo ya kuwauwa Abraham na Wiliam ilikuwa ni lazima ikamilike usiku huo katika misitu ya Mikese mkoani Morogoro,ilikuwa ni lazima awapige risasi za kichwa achimbe shimo na kuwafukia msituni humo, akiamini hakuna hata mtu mmoja angejuwa ni wapi watoto hao wangekuwepo.Alivyofika Chalinze, alikunja kona kulia na kuzidi kusonga mbele ingawa hali ya hewa haikuwa nzuri usiku huo lakini hakujali,wingu lilikuwa zito sana kuashiria kuwa mvua ingenyesha muda mfupi ujao.Ni kweli kwani baada ya kuzikata kilomita ishirini, mvua kubwa ilimiminika ikiambatana na radi kubwa,alizidi kusonga na baadaye aliingia kijiji cha Mikese,akachukua barabara isiyokuwa na rami ambayo ilikuwa na madimbwi mengi ya maji kutokana na ubovu wa njia hiyo,alivyofika mbele kidogo akazima taa za gari kwani msitu aliokuwa anausaka alikuwa ameuona tayari,mvua ilianza kunyesha sio mchezo na radi ilipiga kwa sauti na kufanya hata yeye aingiwe na hofu lakini hakutaka kurudisha moyo nyuma kwani kwa kufanya hivyo Maximo angemnyofoa nyongo, mbali na hapo alihaidiwa mamilioni ya pesa kifupi kwake ilikuwa pesa mbele utu pembeni,akashuka na bastola yake na kufungua mlango wa nyuma.
“Aya njoeni hapa nyie paka”
Wiliam na Abraham walikuwa wamefungwa kamba mikononi,walikuwa ni watoto wadogo lakini walielewa kuwa mbele yao kuna hatari kubwa sana.Kilichowatisha zaidi ni bastola aliyokuwa ameshika mtu aliyefungua mlango wa gari,waliijua kutokana na kuangalia sinema,hivyo walijuwa kwamba inaua!
“Embu shukeni nyie watoto, nimalize biashara yangu niondoke”
Kishoka, alisema bila ya huruma akaingia ndani ya gari na kuwavuta nje,akawaburuza mpaka katikati ya miti mirefu,akawaweka mbele ya mti ili awapige risasi za kichwa.Hakujali kwamba watoto hao ni wadogo tena ni malaika wa Mungu.
“Usituuuwe”
Abraham alisema sababu alijuwa nini kinaenda kutokea.
Akakumbuka shuleni walivyokuwa wanafundishwa kusali na kumuomba Mungu kwenye matatizo, akakumbuka historia kwenye Biblia ya Paulo na Sila walivyokuwa gerezani ,wakaomba na milango ya gereza ikafunguka,akamvuta mdogo wake karibu na kumshika mkono,akaanza kusali sala ya ‘Baba yetu uliye mbiguni’Kishoka hakuwajali, akashika bastola yake vizuri tayari kwa kuwauwa,akaikoki vizuri.Hakuna kitu kilichomshtua Kishoka kama radi kupiga kwa nguvu kama moto na muale wa mwaga kutokea ambao ulipiga mti uliokuwa mrefu kuliko yote,ukakatika katikati na kuanza kudondoka taratibu!



Haikufahamika kama ni Mungu ndiye amesikiliza maombi ya watoto hawa malaika ambao walihitaji msaada wake ama ni muujiza tu, kwani mti ulianza kuporomoka taratibu na kufanya Jambazi huyu Kishoka abaki ameduwaa anaangalia juu,alivyotaka kukimbia akawa amechelewa kwani mti ulimdondokea na kupiga chini, ambapo ulimbana mguu wake wa kushoto,bastola ilikuwa chini kandokando imedondoka,mbali na kudondokewa na mti lakini alitaka kumaliza kazi aliyoanza,akajivuta kwa nguvu kwa shida mpaka alivyoishika bastola vizuri na kuwatizama Abraham na Wiliam,akawanyooshea ili awamalize.
“Pyuuuuu”
Risasi ilipita pembeni,hiyo ilitokana na tawi la mti kumdondokea tena.Hapo ndipo Abraham aliyekuwa kamshika mdogo wake vizuri akaanza kumvuta wakiwa hivyohivyo wamefungwa kamba kwa mbele.
“William,usiogope! Sawa”
Abraham alimtoa wasiwasi mdogo wake,wakaanza safari ya kusonga mbele huku wakikimbia.Walikuwa ni watoto wadogo lakini walielewa nini maana ya kukimbia,walijua tayari mtu waliyekuwa wanampiga chenga ni hatari kwao, ndiyo maana walihofia.Walivyofika mbele, Abraham akaanza kuzing’ata kamba ili zifunguke,bahati nzuri zikaachia akamfungua pia na mdogo wake, Wiliam.
“Twende huku William”
“Kuna giza lakini”
“Wewe twende tu”
Abraham alionekana ni mjanja kuliko mwenzake na walizidi kusonga mbele,mvua iliwanyeshea lakini hawakujali.
Kishoka, alizidi kuuvuta mguu wake kwa nguvu zake zote ingawa alihisi maumivu makali lakini alijitahidi kupambana,akafanikiwa na baada ya hapo akalitupa tawi la mti lililomdondokea,akaokota bastola yake na kuanza kuangaza huku na kule akiwatafuta watoto hao ambao mpaka wakati huo walizidi kumpandisha hasira zaidi na zaidi.
Usongo ukampanda akaanza kufatisha alama za miguu yao ilipopita, kutokana na matope kuwa mengi ilikuwa rahisi kwake kujua ni wapi wameenda.Alivyopiga hatua kama kumi na mbili, alikumbana na kamba ambayo aliwafunga ipo chini,akazidi kuwatafuta huku na kule,kulikuwa na giza totoro hiyo ilimfanya apate taabu kuona.Kilichomsaidia kuona kwa kubahatisha ni mwanga wa radi uliokuwa unawaka kama miale ya kamera.
“Hawa watoto nikiwapata ni risasi tu,sina muda wa kupoteza hawawezi kuniogesha matope namna hii”
Mwili wa Kishoka ulijaa matope mpaka usoni,alichafuka na kujionea kinyaa mwenyewe,kila alipozidi kusonga mbele ndipo alikumbana na miti mingi na vichaka hivyo vilivyomfanya mpaka mwenyewe aanze kusita na kuogopa lakini hakutaka kurudi nyuma, ilikuwa ni lazima amalize kitu alichokianza kwani kwenda kinyume chake angejipunguzia heshima ya kazi kwa Maximo, mbali na hapo angeuwawa kwa kukatwa katwa vipande vipande kama nyama buchani,alivyokumbuka ukatili wa Maximo akapata nguvu ya kuwasaka Wiliam na Abraham,mwanga wa radi uliomulika ulifanya awaone kwa mbele wanatembea, hiyo ilikuwa bahati nzuri kwake na mbaya kwa watoto hawa malaika wa Mungu ambao hawana hatia.
“Kaka Abraham, nimechoka”
William alimwambia kaka yake,humwita kaka sababu Mama yake alimfundisha adabu, humwambia kwamba siku zote amuheshimu Abraham kwa kuwa ni mkubwa wake,safari ya kukimbia ilimfanya ahisi kuchoka.
“Hapana Wiliam,tukibaki tutakufa.Yule ni jambazi ana bastola,una kumbuka movie ya Home Alone Kelvin alivyokuwa anakimbia.Tutege mitego”
Abraham alimtia moyo mdogo wake, wakazidi kusonga mbele hawakujua kwamba tayari wameonekana na muda mfupi wangeenda kukamatwa na kuuliwa.Mbaya zaidi walivyokuwa wanakimbia bila kuona wakajikuta wameingia kwenye tope zito,wakajitahidi kujiburuza taratibu.
“Kaka Abraham,nazama”
“Huwezi kuzama”
“Kaka Abraham,sitaki kufa.Niokoe”
Abraham japokuwa alikuwa bado mdogo lakini alihisi kumuonea sana huruma mdogo wake huyu ambaye alianza kutitia kwenye matope,akazidi kwenda chini mpaka matope yakamfikia kifuani.Abraham alivyotaka kuingia kumsaidia, nayeye akajikuta amenasa, hawakuwa na ujanja mwingine wowote ule kwani walizidi kutitia mpaka matope yakawafunika mpaka usoni kabisa,wakazama!Kishoka alishindwa kuelewa ni wapi tena walipo Abraham na Wiliam kwani muda mfupi alitoka kuwaona eneo alilosimama.Akazidi kuangaza huku na kule bila kuwatia tena machoni,hakuelewa kuwa pembeni yake kushoto ndipo walipokuwa wamefunikwa na matope mpaka kuzama kabisa,bila matope kuwafunika angewaona na kuwauwa hapohapo.
Kuanzia sekunde hiyo mvua ilianza kushuka mara nane yake,ikawa kama Mungu aliye juu Mbinguni badala ya kufungua bomba la mvua akang’oa koki,maji yakaanza kuporomoka kutoka milimani na kushuka chini, hiyo ilimfanya Kishoka aogope zaidi.Hata yeye aliogopa mafuriko hayo,akaanza kutembea kurudi alipotoka kwa taabu sana kwani kulikuwa na matope na maji yalianza kushuka,kifupi yalitokea mafuriko ya ajabu ndani ya dakika chache.
“Potelea mbali inabidi nimwambie bosi,watoto nishawaua.Kwani atajua?”
Wakati akiwa anajaribu kutembea kurudi alipotoka, alitafakari mambo hayo.Ki uhalisia alikuwa ni Mungu anajaribu kuwakomboa malaika wake kwa kufanya wazame kisha baadaye kuachia mvua ambayo ilisukuma matope yakafanya mafuriko,Abraham na William wakaanza kusukumizwa na maji,mpaka walipofika kwenye maporomoko ya maji, hapo alitangulia William kudondoka na baadaye Abraham,hawakuwa na fahamu zozote zile.
**********
“Ebwana pakia mahindi hayo,acha ufala.Hizo gunia ngapi?”
“Gunia tatu”
“Yaani magunia matatu mpaka sasa hivi?Unafanya masihara Luge”
“Hapana bosi”
“Kumbe?”
“Nilidhani wenda hatuendi leo”
“Una kichaa nini”
“Bosi kutokana na wingu kuwa zito”
“Kwani tunatembea kwa miguu?Pakia magunia hayo,kama huwezi sema nitafute utingo mwingine”
Huyu alikuwa mzee Chonga,mfanyabiashara wa zao la mahindi.Ambapo huyatoa Mkoani Morogoro soko la Mawenzi na kuyapeleka Dar es saalam, huko huyakoboa na kuyafunga kwenye magunia kisha kuuza unga.Biashara hiyo ndiyo iliyomtoa kimaisha,hakuwa mzee mwenye mchezo linapokuja swala la kutafuta pesa.Ndiyo maana hata alivyoona kuna wingu zito angani usiku huo hakujali,ilikuwa ni lazima mzigo upakiwe ndani ya Fuso na safari ya Dar es salaam ikamilike.
“Bora Punda afe lakini mzigo ufike!Pakia mahindi hayo”Mzee Chonga akapigilia msumari, akitumia msamiati huo.
Hakukuwa na kipingamizi, vijana wa kazi walipakia magunia ya mahindi ndani ya Fuso na baada ya dakika arobaini na tano mzee Chonga,akaingia nyuma ya usukani.
“Twende bwana,tunachelewa mbona unalegea legea kama mwanamke,Vipi hujala?Unakuwa mzito mtoto wa kiume kama nini,au sio rizki wewe”
Mzee Chongo alikuwa ni mwingi wa maneno na alivyoongea hivyo alikuwa tayari keshalipiga gari moto.Utingo wake akadandia na safari ya kurudi Dar es salaam ikaanza mara moja,hawakufika mbali,mvua ilianza kunya sio kawaida.
Hiyo ilimtia mpaka hofu mwenyewe, kwani alishindwa kuona hata mbele vizuri na kadri walivyozidi kwenda mbele hali ilizidi kuwa mbaya kupita kiasi!
“Inabidi tupaki Mikese,Mvua ikate.Hii Mvua sio ya kitoto naona sasa Mungu badala ya kuweka kifurushi cha halichachi kaachia halikati,hii mvua kiboko.Mpaka gari nalisikia linateleza”
Mzee Chonga aliendesha gari kwa mwendo wa ajuza,alivyofika Mikese akaweka gari kando akisubiri mvua ikate.
Hapo, walisimama nusu saa lizima lakini wapi.Walisubiri mpaka ilivyofika saa kumi na moja kasoro ya asubuhi ndipo angalau mvua ilipungua,gia ikapigwa safari ikapamba moto.Walizidi kusonga mbele.
“Mmmh”
Mzee Chonga aliguna baada ya kuona kitu kimelala barabarani hakuelewa kuwa ni mnyama au binadamu,aliogopa lakini alipunguza mwendo kidogo.Yeye na utingo wake wote wakawa wana kazi ya kutumbua macho yao mbele,wakaweka gari pembeni.Mzee Chonga akashuka na panga ili kujihami na majambazi kwani wakati mwingine huo ndio ulikuwa mtindo wao wa utekaji nyara.
“Huyu si mtoto?”
Utingo aliuliza huku akiangaza huku na kule.
“Ndio,mtoto huyu.Mafuriko haya,sijui huku porini alikuwa anatafuta nini”
“Bosi,msala huu tuondoke”
“Tumuache hapa?”
“Ndio,kesi hii”
“Sasa kesi gani?”
“Mimi nakwambia”
Mzee Chonga na Utingo haraka wakarudi ndani ya gari na kupiga gia.Akiwa nyuma ya usukani anaendesha gari baada ya kutembea umbali wa mita kumi,roho ya huruma ilimuingia kuna sauti aliisikia moyoni inamwambia kwamba msaidie malaika wa Mungu,sauti hiyo ilizidi kumsumbua, hapohapo akaweka mguu kati, Fuso likasimama.
“Bosi mbona umepaki gari?”
“Tunaenda kumchukua Yule mtoto”
Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwani Mzee Chonga aligeuza gari na kurudi, ambapo alimpakia mtoto huyu aliyekuwa barabarani,safari ikaanza moja kwa moja ambapo walivyofika Chalinze walisimama kituo cha polisi,Mzee Chonga akatoa ripoti jinsi ilivyokuwa.
“Huyu mtoto bado mzima mzee,mpeleke hospitali kwanza.Kisha umlete ili tujue tunafanya nini”
Kamishna wa polisi mkoa wa Pwani Afande Kumalija, ndiye aliyetoa pendekezo hilo.
“Sasa sisi tunaenda Dar es salaam”
“Kwani inachukuwa muda gani mpaka Dar?”
“Sawa afande”
Walivyorudi ndani ya gari wakanyoosha moja kwa moja mpaka hospitali iliyokuwa karibu na Chalinze.
Cha kwanza baada ya mtoto huyu mdogo kupokelewa na madaktari, walimpa huduma ya kwanza kwa kumtapisha maji kisha wakamuwekea mtungi wa Oksijeni ili kumsaidia kupata hewa kwenye mapafu ambayo kwa mujibu wa Dokta Okama alisema kwamba mapafu yake bado yana maji.
Nusu saa baadaye,ulikuwa ushindi kwa Dokta Okama, ambaye alitoka huku akiwa amekenua meno yake.
“Ameamka tayari”
“Tunaweza kumuona?”
“Ndio”
Mzee Chonga akaongozana na Dokta Okama mpaka ndani ya wodi ambapo walimkuta Mtoto huyu mdogo analia,anaangaza huku na kule.
“William,William.William yuko wapi?”
Abraham alilia huku akimtaja mdogo wake,ni dhahiri kuwa kumbukumbu zilimjia na alikumbuka walivyokuwa wanakimbizwa.
“Mtoto tulia kwanza.Jina lako nani?”
“Abraham,William yuko wapi?”
“Wiliiam ndio nani?”
“Ndugu yangu”
Abraham alijielezea huku akimwaga machozi na alishindwa kuendelea mbele zaidi.Mzee Chonga hakuwa tena na muda wa kupoteza kwani alilipia bili hospitalini na kumchukua Abraham,alitaka kwanza afikishe mzigo wake jijini Dar es salaam kisha baadaye afanye taratibu za kumuhoji mtoto huyu mdogo na kumfikisha kwa wazazi wake!

***********
Bado Deo aling’ang’aniwa na askari wakidai kwamba wanataka kufanya uchunguzi wa kina, ndiyo maana waligoma kumtolea dhamana,siku hiyo ilibidi alale kituoni.Marietha alibembelezwa ili alegeze uzi, angalau Deo atoke lakini aliweka ngumu,akaweka masikio pamba.Alibakia kuamini kuwa Deo ndiye ana watoto wake na ndiyo maana alimkomesha kwa kufanya kitu hicho na aliapia mambo yasingeishia hapo,angempandisha kizimbani na kumrudisha tena gerezani kama hatosema ni wapi Abraham na Wiliam walipo.
Mpaka usiku Mtui na mkewe walikuwa Kituo cha polisi Urafiki, Shekilango! Wanajaribu kuwaimbisha askari na hata Mtui alipojaribu kutoa hongo ya shilingi laki tatu,ilishindikana askari waligoma kabisa.
Mambo yalikuwa magumu,hawakuwa na jinsi zaidi ya Mtui kutoka pembeni na kununua wali kuku,akaenda nao mpaka kaunta.
“Hajala bado,nimemletea chakula”
Mtui aliwaambia maaskari,ulikuwa ni usiku wa saa tatu tayari na Deo mchana hakula kabisa.Mtui aliingiwa na huruma kupita kiasi ingawa alikuwa bado ana maumivu mkononi ya jeraha la risasi lakini kwa wakati huo hakuyasikia.
“Chakula sasa hivi?Nani kakwambia huu ni muda wa kuleta chakula?”
“Tuongee kibinadamu afande”
“Ubinadamu unaujua wewe?”
“Ngoja nikwambie afande Yule ni binadamu kama wewe.Hizo ni nguo tu basi, ndio maana tunaziheshimu.Unaweza ukanikataza nisimpe chakula leo lakini kesho kutwa tukakutana mitaani.Hiyo kazi uliyonayo ina mwisho wake na kumbuka kuna maisha baada ya hapo.Anyway sawa”
Mtui aliongea kwa hasira,iliyotokana na kuzungushwa huku na kule na maaskari hawa ambao walikuwa wanaonesha dharau,ilibidi afunguke na kama mbwai iwe mbwai,alijisikia kuchoka ndiyo maana aliwatolea povu.
“Alafu unaonekana wewe ni kiburi sana”
“Sio kiburi nakwambia ukweli.Unajiona hapo ulipo upo benki.Namimi katika watu ambao siwaogopi ni askari ukae ukijua hilo sasa.Na siogopi na wala sikuogopi,naomba nikwambie kuwa kesho ama keshokutwa tutakutana huko mitaani”
Afande Chacha alishindwa kujitetea na ilionekana maneno ya Mtui yalimwingia akilini,akashuka na kuwa mdogo kama kidonge cha pilton.
“Aya onja chakula hiko”
Mtui akafungua chakula na kuanza kuonja.
“Onja na huyo kuku”
Hizo ndizo zilikuwa taratibu za mahabusu ilikuwa ni lazima chakula kionjwe kabla ya kufikishwa kwa mtuhumiwa.
Deo aliitwa kaunta na kupewa sahani,kitendo cha kumuona Mtui alijisikia kama kuna kitu kimembana kohoni,alishindwa kujizuia, akaanza kulia kwa sauti kubwa kama mtoto mdogo.
“Deo nyamaza kula chakula,Nyamaza ndugu yangu.Kula kwanza”
Mtui alimfariji lakini hata yeye alijisikia kulia,akajikaza kisabuni.
“Mar..ieth..a ndiyo anani..fanyia mimi hivi?Hapa..na.Ni Mke wangu lakini Yule.Ni mke wangu wa ndoa bora angefanya mtu mwingine.Daaah”
Deo alilalamika huku akipiga piga kifua chake,bado hakutaka kuamini kwamba mke wake wa ndoa ndiye kafanya tukio kama hilo la kinyama,mbali na hapo ni siku chache tu alitoka Jela,hilo ndilo lilimfanya ahisi uchungu zaidi na kuona Dunia imempa kisogo.
“Deo,wewe mwanaume.Hizi ni changamoto tu katika maisha.Siku zote lazima kuwe na usiku na mchana,vuli na masika.Kubali tu,kila kitu kitakwisha”
Mtui alijaribu kumpa moyo rafiki yake.
“Arooo hapa sio ustawi wa jamii,sio mahala pa kupeana ushauri.Kama hali arudi ndani.Muda unakwenda”
Askari mmoja alifoka baada ya kusikia mazungumzo marefu!
*******
Marietha hakutaka kubaki tena jijini Dar es salaam, siku iliyofuata alirudi Tanga na kufika ndani ya nyumba yake akiwa amechoka,mwenye mawazo tani kumi.Bado aliendelea kuamini kwamba Deo ana watoto wake na siku chache tu,angewatoa kutokana na Mzee Maximo kutembeza pesa kituoni huku nyuma yeye akimsisitiza afanye hivyo.Hakuelewa kuwa mzee anayeishi naye ndiye alikuwa mkandarasi wa kila kitu kilichotokea.Baada ya kuoga na kutulia vizuri alimtafuta Mzee Maximo hewani na kumpasha habari kila kitu kilivyoenda.
“Lazima atasema tu watoto walipo,nitakuwa nawewe bega kwa bega Darling nihakikishe kwamba watoto wanarudi”
“Ahsante mpenzi sikutegemea kama ungekuwa na moyo wa kipekee kama huo.Ni Wanaume wachache wenye moyo kama wako.Nitakupenda milele daima”
“Usijali sana watoto wako ni wangu,hata hivyo nipo njiani nakuja huko”
“Sawa karibu sana”
“Ahsante”
Marietha alivyosikia Mzee Maximo atafika,aliingia jikoni na kupika harakaharaka ambapo baada ya chakula kuiva alikitenga mezani,akasubiri dakika kumi nyingine ndipo Mzee Maximo aliingia.
Alimkumbatia na kumpiga busu la mdomo,wote wakapandisha ngazi mpaka chumbani.
“Ngoja nikaoge kidogo,nitoe uchovu”
Maximo akaingia bafuni na kumuacha Marietha chumbani.
“Griii griiii”
Simu ya Mzee Maximo ilianza kuita,akasogea karibu ajuwe ni nani amepiga.Akaona jina ‘KISHOKA’ akaachana nayo, ikaita tena lakini hakupokea sababu hakuwa na tabia hizo,simu ya Maximo ilikuwa ni aina ya ‘IPHONE 6’ meseji ikitumwa inapita juu,ikaunguruma kuashiria kuna ujumbe umeingia, akasogea karibu.
‘BOSS TAYARI NISHAWAUA ABRAHAM NA WILLIAM,KAZI YAKO TAYARI IMEKWISHA UKIPATA UJUMBE WANGU,NITAARIFU’
Huo ndio ujumbe uliosomeka juu ya kioo cha simu ya Mzee Maximo,Mapigo ya moyo ya Marietha yalipiga mkambo na mpaka moyo wake ukataka kutokeza nje ya kifua,akahisi kama amepigwa sindano ya ganzi!


Kitu cha kwanza kumjia ni sura ya Deo akiwa amelowa damu,akahisi kama ni mkosaji mbele za Mungu cha pili ni uchungu uliombana ambao haukuwa na mfano wake,alihisi kujuta kwa kile alichokifanya.Tayari alishajuwa kwamba ‘kikulacho kinguoni mwako’.Alikaa juu ya kitanda bila kutegemea sababu nguvu za miguu zilimuishia,akili yake iliganda, hakuelewa ni kitu gani akifanye kwani watoto wake walikuwa ndiyo kila kitu katika maisha yake na leo hii anasoma meseji ya kwamba wameuliwa, hakuelewa ni kwanini Maximo alifanya hivyo,wakati mwingine alidhani yu ndotoni na muda mfupi angeshtuka, hata hivyo alitamani iwe hivyo kwani hakuelewa ni kwa namna gani angeweza kuishi na jamii ingemchukuliaje kwa ujumla.Machozi ya uchungu yalimtoka na akili ilianza kumjia sasa, kilichomtuma ni kitu kimoja tu,achukuwe simu na kutoa taarifa polisi juu ya kitu alichokiona.Haraka haraka alifanya hivyo na kuchukuwa simu.
“Halloo,naongea na kituo cha polisi Urafiki?Ndio ndio,Deo hakufanya, sio yeye tafadha..li sio yeye naomba mumuachie.Mungu wang…u ndio nina mjua..Ni mzee Maximo,eeeeeh hap…”
Marietha hata siku moja katika mambo yake hakujiongeza wala kutumia akili yake ya kuzaliwa,kwenye swala hilo ilikuwa wazi alikurupuka kwani askari aliokuwa anawapa taarifa walikuwa ni marafiki wakubwa wa Mzee Maximo alafu cha pili,wakati anaongea na kuropoka simuni Maximo alikuwa mlangoni bafuni katega sikio lake anamsikiliza kila kitu.
Kwa maana hiyo, asingeweza kumuacha hivihivi, ilikuwa ni lazima siri yake isivuje kwani ingemuharibia sifa yake na C.V yake ingechafuka, jambo ambalo hakutaka kuruhusu litokee.Akakohoa kidogo na kufungua mlango ambapo alipomuona Marietha anaweka simu kitandani akiwa mwenye hofu.
“Upo sawa Darling?”
Maximo aliuliza makusudi,akitaka kupima maji.
“Ndi..o ndio nipo sawa”
“Mbona kama unalia?”
“Nina mafua”
“Mafua,mara hii ya ghafla.Nikupeleke hospitali?”
“Ha..pana nitaenda mwenyewe”
“Are you sure?”(Una uhakika)
Mzee Maximo alizidi kumdadisi.Hakuna siku aliyoshikwa na hofu kama siku hiyo,Marietha alitetemeka kama mtu mwenye homa ya usiku,hiyo ilitokana na uwoga uliomtanda,ghafla alianza kumuogopa Maximo, ndiyo maana alianza kurudi nyuma na kusogea kwenye pembe ya kitanda akitafakari ni kwa namna gani amkimbie mzee huyu ambaye tayari alimfananisha na shetani mwenye mapembe kichwani.
“Na..taka kwenda dukani mara moja.Kununua dawa”
Marietha alitaka kutumia mwanya huo kukimbia mbali kabisa ingawa hakujuwa ni wapi angeenda, kifupi alitaka kukimbia wakati hana breki!
“Acha nitaenda”
“Ha..pana nitaenda mwenyewe”
Mzee Maximo alitabasamu na kumuangalia mwanamke huyu bwege na fala, ambaye anamzuga ili atoroke wakati yeye alimsoma tayari,alimtizama kwa kama sekunde tatu nzima na kushindwa ni kitu gani amfanye Marietha kwani alimpenda na wakati mmoja alijisikia kumuuwa ili amzibe mdomo wake!
“Naomba niende”
Marietha akaomba tena ruksa!
“Hapana,mimi nimekuja kwa ajili yako”
“Nimebanwa na mafua My Love,wacha niende”
Marietha akalazimisha sababu alisimama na kuanza kutembea kuufuata mlango.
“Mariethaa”
Mzee Maximo akaita,Marietha alivyogeuka alikumbana na mlango wa bastola unamuangalia, hapo ndipo alipohisi kama nguo yake ya ndani imelowana,hakuelewa ni jasho ama ni mkojo.
“Mimi ni mtu mzuri lakini kwa upande mwingine NINATISHA,upande wangu wa pili.Ni mtu ambaye nina roho ya kinyama sana…”
Mzee Maximo akakatisha na kusimama vizuri huku akiwa ameishika bastola yake,akamsogelea Marietha karibu naye kabisa, akamuwekea juu ya maziwa yake.
“Na hao polisi uliowapigia simu,hawatokusaidia chochote kile.Umenielewa?Watoto wako nimewauwa mimi ili niishi nawewe vizuri kwenye hii dunia.Ninakupenda kweli lakini pia ninaweza kubadilika vilevile.Una vitu viwili vya kuchagua,kuishi namimi au kufa”
Kwa Marietha yalikuwa ni mambo magumu kwake kuchagua,alipenda kuishi na Maximo lakini alimuogopa na wakati huo bado alipenda kuishi,hiyo ilimfanya azidi kutetemeka zaidi sababu bastola ya Maximo ilikuwa inapitishwa shingoni tumboni mpaka kwenye ikulu yake,Mzee huyu alikuwa anafanya mambo ya kihuni na alikuwa anasubiri jibu la Marietha ili amtoboe na risasi amuuwe, ama amuache huru.
“Usijidanganye ukatoa taarifa popote pale.Sababu sheria ipo chini yangu”
“Kwa..nini umeamua kuwauwa watoto wangu?”
“Nimekwambia nataka tuishi kwa furaha”
“Hawa..kuwa na hatia yo..yote ile”
“Naona pia ili tuishi kwa furaha inabidi nimuuwe na Mumeo”
“Noooo”
“Yes,ndiyo nitaishi kwa amani na mustarehe nikifurahia penzi letu mimi nawewe.Lakini kazi hiyo nitakupa mwenyewe uifanye kama utapenda kuishi”
Marietha alikuwa kama amepigwa na shoti ya umeme,hakuzungumza tena.
“Niue mimi….Bora uniuwe mimi…Pull the triga”
Marietha alikuwa tayari kufa ingawa kijasho chembamba kilimtoka kwani haikuwa na maana kuishi tena duniani,alijihisi yeye ni mkosaji na hata Mungu asingemsamehee, ndiyo maana alimruhusu Maximo avute kidude kinachoitwa Triga,amuulie mbali.
“Niuwe”
“Niuwe Maximooo,Kill meeeeeeee”
Marietha kwa hasira huku machozi na kamasi vikimtoka,pua zake zinamchesha kifua chake kinapanda juu na kushuka chini,mapafu yake yalijaa hewa!Hakujuwa kuwa mzee huyu ni kichaa na kuna waya mmoja wa kichwani kwake umekatika.
“Kacha kacha”
Mzee Maximo akakoki bastola.
“Paaaaaaaaaa”
Mlio mkubwa wa bastola ukasikika,Marietha akadondoka chini!
********

Asubuhi na mapema Mtui na mkewe walikuwa tayari wamewasili kituo cha Polisi Urafiki, kumpelekea Deo Karekezi kifungua kinywa baada hapo walianza tena kuwaimbisha maaskari ili watoe dhamana,lakini habari ilikuwa ileile, kwamba wasingeweza kufanya hivyo.Lakini cha kushangaza ilivyofika majira ya tisa alasiri,waliitwa na askari na kuambiwa kwamba wanaweza kumchukuwa Deo, kwao hilo likawa kama muujiza fulani hivi.
“Mnaweza kwenda naye”
“Ataripoti tena lini hapa?”
“Haina haja,tushafanya utafiti kwamba sio yeye”
“Ni nani?”
“Usitake kuhoji maswali,nendeni na mtu wenu”
Mtui hakuwa mwenye lingine la zaidi,akamchukuwa Deo,Mkewe pembeni wakaongozana mpaka ndani ya gari na safari ya kurudi nyumbani kwa Mtui,Tegeta kuanza hapohapo.
Ndani ya gari kulikuwa na ukimnya wa ajabu na sauti iliyovunja ukimnya niya mke wa Mtui,akimpa pole Deo.
“Pole sana Shem”
“Nishapoa”
Safari ikaendelea mpaka walivyofika Tegeta.
Kitu cha kwanza aliambiwa akajimwagie maji na kilichofuata hapo ni kunyoosha moja kwa moja hospitali ambapo huko alishonwa nyuzi tatu za uso karibu na paji na nyuzi nne karibu na mdomo wake,matibabu yalivyokamilika, wakarudi na Mtui nyumbani.
“Ahsante sana Mtui”
“Usijali.We are brothers!”
Mtui aliitikia, akimaanisha wao ndugu yaani ni Mtu na kaka yake.
“Sina kitu hata kimoja,mali zangu wamechukuwa.Bado naendelea kuteseka maskini mimi.Sijui nimemkosea nini Mungu”
“Deo,katika maisha epuke kitu kulalamika.Nakuamini sana,wamechukua kila kitu lakini wamekuachia kichwa.Una uwezo wa kupambana.Kitu kimoja nachokuomba kwa sasa hivi kubali kuanza na moja”
Siku hiyo Mtui aligeuka kuwa mshauri wake na alimfariji kwa kumpa moyo na kumtolea mifano mbalimbali ya matajiri waliowahi kufulia na kurudi tena kwenye chati!
“Nakupa mfano ulio hai,kuna ndugu yangu.Mtoto wa Shangazi yangu anaitwa Alex Masawe nadhani unamjua”
“Yupi huyo?”
“Kuna kipindi nilikuwa naye sana beneti,mara ya kwanza unafungua baa yako nikaja naye.Anatembelea Range Rover nyeupe”
“Nishamkumbuka”
“Yule jamaa kuna kipindi alifisilika alifulia vibaya,akataka mpaka kujiua”
“Ilikuwaje?”
“Alikuwa Marekani,anafanya kazi anatuma pesa Tanzania kwa mkewe ili anunue kiwanja wajenge nyumba,bwana weeee….”
“Enhee ilikuwaje?”
Deo alikaa sawa ili asikilize mkasa huo.
“Jamaaa akatuma mara ya kwanza dola elfu moja.Akamwambia mkewe anunue kiwanja,baada ya miezi mitatu akatuma tena pesa mke wake aanze kujenga nyumba.Sasa cha ajabu Yule mkewe akawa anamtumia picha kweli kama ushahidi kuwa nyumba ishaanza kujengwa.Baada ya miaka miwili Mkewe akamtumia picha Masawe,bonge la jumba”
“Ikawaje sasa?”
“Alivyorudi akakuta hakuna hata kitu kimoja hakuna kiwanja wala kitu gani….”
“Mungu wangu…”
“Masawe alichanganyikiwa unaambiwa,alimsaka Yule mwanamnke ili amuuwe.Mimi nikamzuia,nikamwambia haina maana.Masawe alikaa miaka miwili Moshi,kachoka akawa kama chizi mchaafu sana”
“Sasa hivi yuko wapi?”
“Sasa hivi ana pesa sana”
“Anafanya shuguli gani?”
“Alienda Mererani kwenye migodi kule, kufanya kazi baada ya miaka minne,akafungua kiwanda cha kuuza mafuta ya petroli”
“Duu”
“Wiki ijayo ukimaliza dozi,nitakupeleka sehemu moja hivi tukalewe kidogo”
Siku ziliendelea kwenda adoado na hatimaye wiki ikakatika kimasihara na hata siku moja Deo hakuwahi tena kumzungumzia Marietha,kitu kilichokuwa kinamsumbua kichwani ni damu yake, Abraham.
Aliamini yupo mahali fulani anateseka lakini hakujuwa ni wapi kwani aliambiwa alitekwa nyara,yote hayo alimuachia Mungu!
“Deo twenzetu basi”
“Ndio namalizia kuvaa hapa”
“Poa,fanya haraka”
Siku hiyo ilikuwa ni siku ya Ijumaa saa moja kasoro robo jioni,Mkono wa Mtui pia ulikuwa kidogo una nafuu na alimaliza dozi ndio maana alihisi amebanwa na kiu ya kupiga masanga,hakutaka kwenda peke yake ilikuwa ni lazima aende na Deo wakafurahie maisha na huko niya yake ilikuwa ni kumkutanisha na matajiri wengine ambao wamgempa mwanga wa kusimama upya.
“Tunaenda wapi sasa?”
Deo aliuliza baada ya kuingia ndani ya gari.
“Story za kway Grocery”
“Story za Kway Grocery?”
“Ndio,vipi?”
“Huyo Kway.Kway yupi?”
“Mchaga fulani hivi mjanja mjanja hapa mjini”
“Au Kway mwingine?”
“Wewe unayemjua ni yupi?”
“Nilisoma naye Primary”
“Moshi kuna Kway wa Kibosho na Marangu.Au unasemea huyu Mtunzi Emmanuel F.Kway?”
“Huyo huyo”
“Sasa hapo napoenda ni kwa mdogo wake lakini alimuuzia hisa yaani alinunua hisa kwa kaka yake,ni shareholder lakini grocery ya huyohuyo Kway unayemfahamu”
“Duuu,wachaga nyie kwa kubebana”
“Wachaga tuna upendo sana.Ngoja nikupeleke kwa huyo Mdogo wake anaitwa Brian.Ni mtoto mdogo tu lakini kina pesa, kaka yake ndio kamfundisha biashara,nachompendea yeye yaani muda wote anatafakari njia za kutafuta pesa.Utasikia Mtui hivi kwanini tusitengeneze night club,mara Mtui kwanini tusifungue kiwanda chetu cha Bia..Yaani acha,utamuona”
Stori ziliendelea huku Mtui akiwa makini nyuma ya usukani,walivuka Mataa ya Ubungo na kunyoosha moja kwa moja, ambapo walivuka Riverside,wakapita External,Kituo kinachoitwa Garage wakakivuka na kukunja kona baada ya kufika kituo cha mafuta cha Camel,wakasogea mbele kidogo na kusubiri.
“Brian yupo leo.Naona gari yake”
“Gari yake iko wapi?”
“Hiyo hapo, Prado”
Wote wakashuka na kutafuta kona ya mwisho,watu walikuwa wengi kiasi.Mhudumu mmoja mrembo,aliyevalia kimini alisogea karibu kuwasikiliza.
“Niletee Kilimanjaro ya Moto”
Mtui akaagiza.
“Kaka?”
“Serengeti ya Baridi”
“Alafu samahani dada”
Mtui akamsimamisha Mhudumu.
“Naniiii,Brian Kway yupo?”
“Ndio”
“Yuko wapi?”
“Yupo kule Kaunta”
Mtui akasimama na kutembea mpaka ndani Kaunta,ambapo huko alimkuta kijana huyu maji ya kunde mnene kiasi,amekaa anachat na simu.Akamshika Bega!
“Mtuiiiiiiii,ayayayayayaya..Mtui Mtui Mtui Mtui Mtuiiiiiii.,Mtu mubaya wewe,umenitupa sanaaaa”
Brian alivyomuona rafiki yake, alimchangamkia na kumkumbatia huku akimpiga piga mgongoni.
“Linaaa,huyu bili yake weka kwangu sawa.Umekaa wapi Mtui?”
“Nipo pale nje na rafiki yangu”
“Embu twende”
Wote wakaongozana mpaka nje ambapo,utambulisho ulianza.Deo alitambulishwa na wote wakaanza kunywa pombe!
“Hivi Emma yuko wapi?”
Deo alimtupia Swali Brian.
“Nani kaka angu?”
“Ndio”
“Yupo Nairobi.Unamfahamu?”
“Ndio,nilisoma naye”
“Anyway.Mtui bwana juzi hapa si walikuja askari mzee,nikapigwa Pingu”
“Wachaaa, kwanini?”
“Baa ilikuwa wazi mpaka saa saba, wakaja na difenda.Kuna kitu kimoja nimejifunza siku hizi,ukiwa mfanyabiashara pingu ni kitu cha kawaida sana”
Sentensi hiyo kutoka kwa Brian, ilimfanya Deo ajifunze kitu.
“Pingu na mfanyabiashara ni marafiki, kwahiyo hata siku moja Mtui usiogope,kwanza nilivyofika kule Lockup nikawa natabasamu.Kwa sababu mwanaume huwezi kuwa mwanaume kama hujalala kituo cha polisi.Hata broo alivyokuja kunitoa nikamwambia embu niache kwanza”
Siku hiyo waliongea vitu vingi sana na Deo alikuwa anajifunza kupitia mazungumzo hayo.
“Lakini huwezi kufanikiwa hata siku moja kama huna Baraka za wazazi,iwe mama au Baba!Sisi wachaga watu wengi wanasema sijui tunaenda kutambika mara kutoa kafara kila December,which is very wrong.Kule tunaenda kuchota Baraka kwa wazazi,kwa bibi na babu zetu.Ndio maana kila tukifanya kitu kinafanikiwa.Hakuna Baraka njema ama zinazoishi kama za Baba na Mama,kama uliwakosea wazazi wako ndugu yangu.Hutofanikiwa utaishia kusema umerogwa”
“Hilo nalo ni kweli”
“Kuna wanaume mafala sana alafu,wapumbavu hawana akili eti anamtukana Mama yake kisa mwanamke.Mama yako amekuweka tumboni miezi tisa,kakulea,leo umefanikiwa unamtukana na kumdharau.HUWEZI KUFANIKIWA HATA Kidogo na kama ulikuwa una pesa ni lazima utafirisika tu.Amini usiamini”
Deo alijishtukia na moja kwa moja alihisi kama anasemwa yeye, kwani mara ya Mwisho alimtukana Mama yake mzazi,kuna taa nyekundu iliwaka ndani ya kichwa chake kwamba ni moja kwa moja kuwa mambo yanayotokea ni laana kubwa kutoka kwa Mama yake,hivyo ilikuwa ni lazima arudi Bukoba akaombe msamahaa kabla ya kufanya kitu chochote!
Siku hiyo walivyotoka hapo usiku alimshukuru sana Mtui kwani kuna somo alijifunza,usiku huo huo akaomba nauli ili aende Bukoba, kuomba msamahaa kwa Mama yake mzazi,hakukua na kipingamizi chochote!
Nauli ikatolewa na kulivyokucha bila ya kupumzika Deo alienda Ubungo na kupanda basi kwa safari ya kwenda Bukoba,kijiji cha Ngala!Basi lilitembea barabarani kwa takribani siku mbili,walilala Kahama na kulivyokucha,safari ikaanza tena upya!
Alifurahi kufika salama asubuhi hiyo na alikuwa na kibarua kizito kwani hakuelewa kama Mama yake angemsamehe ama la,sababu ni miaka mingi sana ilipita bila ya kuwasiliana naye.
********
Kila alipozidi kupiga hatua,nguvu zilizidi kumwisha kwani nje ya nyumba yao kulikuwa na turubai.Watu wamejaa nje,wanawake wanalia.Alihisi kuchanganyikiwa mno.Aliomba Mungu kitu anachokiwaza kisiwe cha ukweli,ndiyo maana alisogea taratibu mno!Kwa mbali alimuona mdogo wake wa tumbo moja,Eveline.Akasogea taratibu!
“Kakaaaaa Deoooo”
Eveline alimrukia Kaka yake na kuanza kumwaga machozi.
“Maaaamaaaaaaaa……Mamaaaaaa uwiiiii Deooo”
Eveline alimwaga machozi huku akiita Mama.Deo alihisi kuchanganyikiwa zaidi na zaidi,akahisi kama mwili wake umepigwa sindano ya ganzi.



Mabalaa yaliyomtokea Deo Karekezi yaliambatana mfululizo, aliyachukua moja kwa moja wenda ni laana kutoka kwa Mama yake mzazi, ambaye alimtukana kipindi cha nyuma alivyokuwa ana uwezo kifedha,miaka hiyo alivyokuwa anabadili magari ya kifahari na kuruka viwanja anavyojisikia kwenda.
Mambo hayo yote yalibadilika ghafla, tena yaliambatana na matatizo lukuki ikawa kinyume chake kiasi kwamba alianza kubadilisha matatizo kama nguo,leo likitoka hili kesho anavaa lile.Leo hii yupo Bukoba,kijiji cha Ngala niya na madhumuni yake ni kumuomba Msamahaa Mama yake mzazi akiamini kwamba akifanya hivyo ataishi kwa amani.
Kitu kilichomchanganya zaidi ni baada ya kuona Turubai nje ya nyumba ya Mama yake huku kukiwa na mkusanyiko wa watu wanalia,picha iliyomjia kichwani ilimtisha mwenyewe!
Jambo lililompa jibu la maswali aliyokuwa anajiuliza ni baada ya dada yake anayeitwa Eveline, kutokea akiwa analia machozi ya uchungu huku akiita ‘Mamaaa’Hiyo ilimfanya ahisi nguvu zake za miguu zinakosa stamina!
“Mama amefarikiiii De…o uwiiiii”
Eveline alikuwa akilia kwa uchungu akiwa amemkumbatia Kaka yake Deo,ambaye hata yeye alionekana alishindwa kuvumilia,machozi yakaanza kumdondoka akahisi uchungu ajabu, safari aliyofunga kutoka Dar es salaam mpaka Mkoani Bukoba, ilikuwa ni bure.
“Alifanya nini?”
Deo alijikakamua na Kuuliza.
“Ali..umwa na nyoka akiwa shambani”
Eveline alijibu kwa kwikwi huku makamasi yakimtoka!
“Maskiniii Mama yanguuuuuuuu”
Deo alipaza sauti na kudondoka chini huku akilia kwa sauti,wanaume wenzake waliokuwa nje walisogea karibu na kumuinua,wote walimshangaa sana wakajitahidi kumtuliza na kumpa moyo!
“Evelineeee”
Sauti ya Mwanamke mmoja kutokea ndani ilimshtua Eveline, aliyekuwa katikati ya watu analia.
“Mama yako anakuita”
Neno hilo lilipenya moja kwa moja kwenye ngoma za masikio ya Deo, hakuelewa kama alisikia vibaya ama anaota lakini alimtizama Eveline kwa macho fulani ya kutaka kujuwa kitu,akatembea mpaka karibu yake.
“De…o twen..de ukampe pole Mama”
“Mama gani?”
“Mama,Mama yetu”
“Eveline mbona sikuelewi?!”
“Mama mdogo Angela amefariki”
Deo alimwangalia Mdogo wake na kushindwa kuelewa vizuri lakini ilibidi amfuate nyuma nyuma mpaka walipofika seblen,akaangalia kushoto na kumuona Mama yake mzazi yupo kwenye kona ya mwisho, amezungukwa na wanawake wanamtuliza asilie.Moyo wake ulipiga kwa nguvu kwani fikra zake zilimtuma wenda hatumuona tena Mama yake.Akawasalimia wakina Mama wote lakini alivyomfikia Mama yake hakuitikiwa.
“Shikamoo Mama”
Deo akatupa salamu tena kwa mara nyingine lakini ilidunda,Mama akageukia upande wa pili.
“Mama Shikamoo”
Akarudia tena.
“Deo,mwache kwanza Mama yako.Baadaye mtaongea”
Sauti hiyo ilitoka kwa Mwanamke mwingine aliyekuwa upande wa kushoto wa Mama Deo,swala la Mama yake kukaa kimya lilimuumiza sana mtima,hakuwa na jinsi zaidi ya kutoka nje.
*******
Siku zilijisogeza mbiombio, hatimaye wakamzika Mama yake mdogo ambaye walikuwa wakiishi naye hapo.Hata baada ya msiba kuisha Deo alivyojaribu kumfuata Mama yake ili wazungumze ilishindikana.Ilibidi amtafute Eveline na kumtoa pembeni amueleze hali halisi ilivyokuwa.
“Nitaenda kuongea naye lakini sijui kama atanielewa sababu hataki hata kukusikia Kaka Deo”
Eveline,akanyoosha moja kwa moja mpaka chumbani kwa Mama yake na kumueleza,akijaribu kumuombea Deo msamahaa.
“Sina mtoto anayeitwa Deo,nilishakwambia Eveline”
“Lakini Mama,kaka Deo amekuja kukuomba Msamahaa”
“Eveline,ondoka chumbani kwangu”
Kwa kitendo alichomfanyia Deo miaka iliyopita kipindi alivyomfuata Dar es salaam, ilitosha kabisa kuapia kwamba hatokuja kumsamehe na alishasema kuwa hana mtoto tena anayeitwa Deo,huo ndio ulikuwa msimamo wa Mama huyu wa kihaya!
“Eveline”
Mama akaita baada ya Eveline kugusa mlango akitaka kuondoka.
“Abee Mama”
“Mwambie sitaki kumuona hapa nyumbani,arudi alipotoka.Yeye si alinifukuza Kwake namimi namfukuza kwangu”
“Lakini Ma…”
“Au nije mwenyewe kumfukuza?”
“Mamaaaa..”
“Eveline.Huyo kiumbe mwambie atoke sasa hivi”
Maneno ya Mama huyu yalimaanisha na Eveline alielewa nini maana yake endapo angesimama na kutoka kumfukuza Deo kwani asingetumia ustaarabu, kitu ambacho hakutaka kitokee.
Alichofanya Eveline ni kumtafuta Deo na kupunguza ukali wa maneno.
“Amesema atakusamehee lakini leo hayupo sawa”
“Yupo chumbani kwake?”
“Ndio”
“Ngoja nikamuone”
“Hapana Deo”
“Eveline acha niende”
Deo akapiga moyo konde,akatembea kwa hatua chache mpaka mlangoni kwa Mama yake,akagonga.Bila kukaribishwa akaingia na kudondoka kwa magoti.
“Mamaaaa”
“Mamaaaa.Mamaaaa Mwanao nimerudi nahitaji msamahaaa wako,nimekosaa”
Mama alivyomuangalia Mwana kuna kitu kilimrudisha nyuma kwa kasi ya roketi,akakumbuka alivyotimuliwa.
“Yametimia sasa.Nilikwambia utakuja Bukoba ukiwa umepiga magoti”
Deo aliikumbuka Sentensi hiyo, akaanza kumwaga machozi,maneno aliyoambiwa na Mama tayari yalitimia.
“Mamaaa naomba nisa..mehee”
“Deo,ondoka kwangu.Mimi sio Mama yako tena,nenda kamtafute Mama yako”
“We..we ndio Mama yangu,ndio maa..na nipo hapa.Dunia isha..nifunza Mama..Ulimwengu ume..nifunza Mama nipokee Mwa..nao”
Deo alilia machozi ya kwikwi.
“Si una baba,nenda”
“Siw..ezi Mama.Naku..penda Mama ya…ngu ta..fadhali naomba uni..samahee”
Deo alilia kama mtoto mdogo, aliyefiwa na wazazi wake wote wawili,Eveline alitokea nyuma yake alimuonea huruma nayeye akajikuta analia machozi ingawa hakuelewa ni kwanini,ila alihisi uchungu wa hali ya juu sana!
“Baba yako,alinitelekeza.Nilikulea kwa uchungu Deo.Niliuza Senene pekupeku ili wewe usome nikajua wewe ndio utakuja kunifariji kumbe nawewe ni kama baba yako…..”
“Ma..ma usiseme hiv..yo!Na..omba unisa..mehe”
“Deo nenda,siwezi kukusamehe.Naomba niache nipumzike”
Deo hakutaka kubanduka ndani ya chumba cha Mama yake na Mama hakutaka kumsamehee na aliendelea kumwambia kwamba atoke chumbani kwake,ilikuwa ngumu kwa Deo kufanya hivyo.
Muda ulizidi kwenda na ilivyofika usiku wa saa mbili, ilibidi atoke ingawa hakusamehewa.
“Na sitaki kukuona kwangu,washa gari lako ondoka.Safari njema”
Mama aliongea maneno hayo akidhani wenda bado Deo ana gari sababu siku zote anapoendaga Mkoani hapo, ilikuwa ni lazima afike na gari yake.Hiyo ilimtonesha vidonda,akatoka nje na kwenda kusimama kibarazani ambapo hapo alianza kulia mtindo mmoja,mbaya zaidi mvua ilianza kunyesha,mlango ulikuwa tayari umefungwa, asingeweza kuingia ndani, hivyo mvua ilimnyeshea kupita kiasi.
Eveline alijisikia huruma,alitamani atoke nje amwambie kaka yake aingie ndani lakini hakuweza sababu funguo za Mlango alikuwa nazo mama yake.

SIKU ZOTE DAMU NI NZITIO kuliko maji na Mama atabaki kuwa na upendo wa kipekee kwa Mwanaye,ingawa alimfukuza Deo na kumwambia hatoweza kumsamehee lakini moyo wake ulimuuma mno akiwa kitandani,ilikuwa ni saa saba ya usiku tayari!Akainuka kitandani na kuingia chumba cha Eveline, ambapo alimkuta bado analia.
“Mamaaa..Msa..mehee Ka..ka Deo”
“Yupo wapi?”
“Yupo nje,analowa..na na mvua”
“Shika funguo nenda kamfungulie mlango”
Deo akafunguliwa mlango,alikuwa amelowa chapachapa lakini hakujali,akamwangalia Mama yake huku akivuta kamasi.
“Mwanangu Deo na Eveline njoeni”
Mama aliwaita wanaye na kuwakumbatia huku nayeye akilia kwa sauti.
Hapohapo alitoa msamaha na kumwambia Deo kuwa anampenda sana.Wote walikuwa wakilia ilikuwa kama msiba siku hiyo,hatimaye Deo akasamehewa!Nayeye bila kuficha kitu chochote aliweka kila kitu wazi na shida zote alizopitia,hakuacha kitu chochote kile nyuma kuhusu maisha yake,mpaka alivyopelekwa jela!
Ilikuwa ni historia ya kuuzunisha kuliko yoyote ile ambayo waliyowahi kuisikia, hakuna hata mmoja kati yao aliyekubali kwamba Deo kufumba na kufumbua amekuwa, ohehahe!
“Pole sana Mwanangu.Mkeo nayeye yuko wapi?Mwite nayeye mje kukaa hapa nyumbani”
Kidonda kilichokuwa kinaanza kukauka kilianza kuchokonolewa na sindano,swali hilo lilimtonesha Deo kidonda!Akatizama chini kidogo kisha kumuangalia Mama yake usoni.
“Deo,mkeo yuko wapi?”
Yalikuwa ni machungu yaliyozidi kipimo chake,ilikuwa ni lazima aseme yaliyomsibu ingawa siku zote alikuwa ni msiri kuhusu mambo yake ya ndani.Akaanza taratibu kuongea tangu alivyoachana na mwanamke aliyeitwa Leila baada ya kumkuta na vibuyu chumbani kwake,akasogea mbele kidogo akahadithia jinsi maisha ya ndoa yalivyokuwa matamu kwake,alivyosafiri na Marietha mpaka Ufaransa!
Majanga yote yalivyomkuta akiwa safarini,akarudi Tanzania akakumbana na mabalaa mengine.Hakuacha kusema namna alivyotimuliwa na Marietha,hiyo ilimuuma zaidi na zaidi.Alivyomkumbuka mtoto wake Abraham ndiyo alihisi kama kifua chake kinaunguzwa na moto!
“Mwana..ngu sijui alipo Mama.Mbaya zaidi Ma..rietha aliniletea polisi Mama,akaniweka ndani si..ku moja.Sitokuja kusahau Mama”
Deo alihitimisha huku akilia, kamasi zikawa zinamchuluzika mpaka mdomoni.
“Ndio Dunia ilivyo mwanangu.Hayo ni majaribu ya Dunia.Wewe ni Mwanaume,jikaze.Mungu yupo mwanangu”
Siku hiyo uligeuka na kuwa msiba mwingine na usiku huo hakuna mtu aliyelala.

***********
Hakuna watu waliocheka na kufurahi kama majirani walivyoona Deo kafirisika na kurudi kijijini akiwa hana kitu,hiyo iliwapa nafasi ya kuongea na kila mtu alisema yake kijijini hapo.Wengine walisikika wakisema nyuma ya utajiri wa Deo kulikuwa na nguvu za giza,wengine wakasema kwamba Deo ni Freemason,wanakijiji wengine wakavuka mipaka na kudiriki kusema Deo ndiye aliyemuua Mama yake mdogo na kumtoa kafara!
“Kailembo,unamuona huyo jamaa hapo Dukani?”
Sauti ya mlevi mmoja, ilisikika akiwa kirabuni baada ya kumuona Deo amefika dukani.
“Ndioo”
“Huyu ndio Deo,Mtoto wa Mzee Karekezi.Ujue maisha haya niya ajabu sana”
“Kwaniiniii?”
“Huyu jamaa,alikuwa ni tajiri saaana.Unajua tajirii nikikwambia sijui kama unanielewa.Ngoja nikupe mfano unielewe,alikuwa ana uwezo wa kupanga elfu kumikumi hapa mpaka Malawi na chenji ikabaki”
“Weeeee,ikawaje sasa?Mbona yupo hivyo?”
“Pesa za uchawi hazidumu,alikuwa ni mshirikina sana.Pesa za mashetani hata siku moja hazikai.Alishindwa Masharti”
“Sindo huyu niliambiwa juuzi hapa na Denisi kwamba alikuwa sijui…Ninini Mansoon”
“Freemason”
“Hiyo hiyo”
“Sindo huohuo uchawi wenyewe.Ndiyo kamuuwa Mama yake mdogo.Mungu naye akamuonesha,ndio hivyo unavyomuona hapo kachoooka hata senti moja hana wakati alikuwa ana mpaka helkopta binafsi huko Dar.Sasa hivi hana mbele wala nyuma”
Hivyo ndivyo ilivyokuwa,kila mtu aliongea neno lake wakijifanya wanamjua sana,walivyojaribu kuunganisha matukio iliwafanya waamini asilimia mia moja kwamba Deo Karekezi nyuma ya utajiri wake,kulikuwa na nguvu za giza na baadaye alikosea masharti ndiyo maana aliyumba na kuangukia pua.Maneno hayo yalimfikia,aliumia sana lakini hakutaka kuongea chochote kwani alijua kuwa hawezi kushindana na waliwengu sababu hata ufanye nini ni lazima wataongea tu.
Kilichomjia kichwani kwake ni kuanza biashara lakini hakujua ni ipi na hakuelewa ni wapi angepata pesa ya mtaji!Alifanya uchunguzi wa kina na kuamua kujikita kwenye kilimo cha mazao ya mahindi,huko ndipo alipoamini kwamba atapata angalau mkate wake.Hakutaka kukaa na wazo hilo kichwani,hapohapo alilifanyia kazi,akamtafuta dada yake Eveline na kumueleza mchakato mzima!
“Niazime laki tano,nitakulipa Eveline”
“Laki tano? Mimi nitaitoa wapi Kaka Deo?Mimi ni mwalimu.Hapa nina akiba tu ya laki mbili”
“Nitakulipa,nisaidie hata kuomba mkopo”
“Deo ninaogopa maswala ya mikopo mimi”
“Usiogope mdogo wangu.Niamini”
Mtu na mdogo wake siku hiyo waliteta.Eveline alikubali na alivyofika shule aliyokuwa anafundisha,alinyoosha moja kwa moja kwenye uongozi wa Shule,akaomba mkopo na kupatiwa baada ya wiki moja baadaye.
Akarudi na kumkabidhi Deo!
Kichwani kwa Deo kulikuwa na mipango mingi, hakutaka kukurupuka,alichofanya ni kuanza kuulizia elimu ya mazao hayo ya Mahindi inavyokuwa kuanzia kulima mpaka uvunaji wake na mwisho akaulizia jinsi yanavyouzwa.
“Hapa lazima nitumie FIFO au LIFO”
Kichwani kwake ilimjia njia hiyo ambayo alifundishwa kipindi anasoma somo la Uchumi chuoni,akachambua akaona bora atumie nyenzo ya LIFO yaani Last in First Out!Kwa elimu aliyokuwa nayo aliamini kwamba ni lazima miezi minne baadaye atafanikisha ndoto yake ya kuuza mahindi.
Alichofanya kitu cha kwanza ni kuandika kila kitu juu ya daftari lake.
“Miezi mitatu baadaye nitalipa deni la Eveline mambo taratibu taratibu,kisha faida itakayopatikana sitoigusa nitanunua magunia mengine ya mahindi kisha nitasafirisha Kahama kule kuna uhaba wa chakula”
Mwanaume huyu hakulaza damu na alijiamini hiyo ndiyo ilikuwa nguzo yake,kulivyokucha asubuhi yake, akakodi baiskeli mpaka kijiji jirani ambapo huko alinunua magunia ishirini ya mahindi,akapitia duka la madawa, akanunua pia na dawa ya kunyunyizia mahindi yasiharibike,pesa iliyobaki alimpatia fundi ajengee gala la kuhifadhia magunia hayo ya mahindi.
Shabaha yake ilikuwa moja tu,baada ya miezi miwili ayapeleke Bukoba Mjini,akauze kwa tshs 1000/- kisado,wakati yeye alinunua kwa tshs 300/-Hiyo ingekuwa faida kubwa sana kwake.

***** ******
Abraham alizidi kukuwa kwa Kimo na hekima,Mzee Chonga ndiye alikuwa mlezi wake na alimpenda kama mwanaye wa kumzaa.Hata mkewe pia aliyefahamika kwa jina la Verynice,alitokea kumpenda sana mtoto huyu kuliko hata anavyojipenda yeye.
Mwaka ukakatika kimasihara na Abraham alijihisi kuzoea akajikuta amesahau kwa haraka jinsi alivyotaka kuuwawa ingawa hakuweza kumsahau mdogo wake William.
Akaanzishwa shule nyingine ambapo alipewa elimu ya shule ya msingi,bado uzuri wake uliendelea kuwa tishio kwa yoyote aliyemuona!Kifupi alikuwa Homa ya mtaa,kadri miaka ilivyozidi kwenda,sauti yake ilizidi kubadilika ikaanza kukwaruza na alijihisi hali ya tofauti kabisa katika mwili wake,alivyofikisha miaka kumi na saba ndio usiseme, ilikuwa ni wazi kuwa anapitia katika balehee.
Kila kiungo chake kilitanuka licha ya yote Abraham alikuwa ana mapozi ya kuongea na aliweza kuyapangilia maneno,alikuwa anaongea taratibu mno hiyo ilifanya wasichana waanze kujisogeza kwake karibu,kifupi walimshobokea.Kila msichana aliyekuwa anasoma naye,alitamani awe wake.Lakini kilichowafanya wasichana hawa wamuogope ni kutokana na majibu yake,Abraham alikuwa mwenye majibu ya mkato,kifupi hakutaka shobo!
“Abraham,mbona jana nimekuomba tuonane.Hukufanya hivyo?”
Hiyo ilikuwa sauti nyororo kutoka kwa msichana aliyeitwa Veronica, alikuwa ni msichana mrembo mno nayeye alikuwa miongoni mwa wasichana walioteseka kumpata Abraham lakini siku hiyo hakutaka kulaza damu, baada ya kutoka darasani akamfuata na walikuwa wanasoma wote kidato cha tatu lakini madarasa tofauti.
“Ulitaka uonane namimi?”
“Ndio,kwani hukuona barua yangu?”
“Huwa siitwi kwa barua, kama una shida namimi nione direct”
“Nina mazungumzo nawewe”
“Nakusikiliza Veronica,nina haraka hapa”
“Nipe dakika moja tu Abraham”
“Dakika moja ishaisha mbona”
Abraham akataka kuondoka,Veronica akamshika mkono!
“Abraham,unanitesa.Unanitesa sana.Unaunyanyasa moyo wangu nionee huruma”
Veronica,akafunguka lakini alizunguka kidogo mbuyu!
“Mimi,naunyanyasa moyo wako?”
“Ndio Abraham,nakupenda sana”
“Namimi nakupenda mbona”
“Sio hivyo unavyodhani”
“Kumbe?”
“Naomba uwe mpenzi wangu”
Veronica akazidi kuongea kwa hisia kali sana,hakuelewa kwamba anaonwa na Mwalimu Beatrice ambaye hata yeye alitokea kumpenda mwanafunzi wake Abraham ingawa alikuwa ni mkubwa kwake lakini hilo hakujali.Alihisi wivu na kuanza kutembea kuwafuata walipo!



“Mnafanya nini hapo?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Mwalimu Beatrice wa somo la Biology,kitendo cha kumuona Abraham kasimama na Veronica kilimuuma na alihisi wivu.
“Nilikuwa nataka kumuomba daftari lake la Kiswahili,nikopi notes”
Beatrice akajibu.
“Kwani wewe huna daftari?”
“Ninalo lakini sikukopi notes”
“Ulikuwa wapi?”
“Nilikuwepo darasani laki..”
“Lakini nini?Embuu njoo ofisini ukamueleze huo upuuzi Mwalimu Macha.Nimekwambia twende ofisini Vero.Wazembe kama nyie ndio nawatafuta”
Hakuwa na sababu yoyote ile ya kumchongea kwa mwalimu wa somo la Kiswahili, alifanya hivyo kutokana na kuendeshwa na wivu uliomuingia.Ni kweli,hakutania kwani alimpeleka moja kwa moja ofisini na kupeleka unoko kwa walimu wengine.
“Alafu una notes zangu za Biology?”
Mwalimu Beatrice akazidi kumkandika Veronica maswali.
“Ndio ninazo”
“Toa nione”
Hivyo ndivyo ilivyokuwa siku hiyo, Mwalimu Beatrice alikuwa kama trafiki wa barabarani anayetafuta makosa,ilimradi tu amuhadhibu viboko na hivyo ndivyo ilivyokuwa kwani Veronica alikutwa na makosa, akapigishwa magoti,akacharazwa viboko.
Kesho yake asubuhi alinyoosha kwa Abraham na kumueleza kila kitu kilivyokuwa.Na bado hakukoma kumsihii amkubalie ili wawe wapenzi.
“Naelewa hata Blandina anakutaka.Lakini Abraham naomba nihurumie mimi nakupenda kweli”
“Veronica,embu usipoteze muda wako.Mimi siwezi kuwa nawewe”
“Kwanini sasa?”
“Sina jibu la kukupa lakini ndio ujue hivyo”
“Abraham tafadhali”
“Tafadhali nini?Jaribu kuwa mwelewa,mimi sikupendi na huwezi kuwa namimi”
“Kwanini lakini?”
Veronica akauliza kwa masikitiko makubwa sana sababu hakutegemea majibu hayo kutoka kwa Abraham,mbali na hapo alishindwa kutafakari Abraham angemchukuliaje kwani haikuwa desturi kabisa kwa msichana wa kiafrika, kumtongoza Mwanamme!
“Usinichukulie kama malaya Abraham”
“Usijali”
Huo ndio ulikuwa msimamo wa Mvulana huyu,Veronica alitumia kila njia anazozijua yeye ili kumsogeza karibu lakini wapi alichomolewa na kupigwa kibuti.
Na mara nyingi aliendelea kutuma barua lakini hazikujibiwa.
“Abraham,barua yako hii”
Siku hiyo saa kumi ya jioni baada ya kengele ya kutoka darasani kupiga,alipokea barua kutoka kwa rafiki yake ambaye walisoma darasa moja aliyeitwa,Lazaro Saranga.
“Nani kakupa?”
“Vero”
“Dah!Alafu huyu demu bwana.Anakuwa hasikiii mimi simtaki msumbufu kweli yaani”
“Kaka,usilembe.Mtoto mzuri kama yule unamwacha vipi?Gonga ngozi”
“Ah,bado hajanivutia.Demu gani Yule wa kutoka namimi”
“Acha masihara,hapa shule nzima kila mtu anataka kuwa naye.Hivi upo sawa Abraham?Hiyo bahati ningeipata mimi hakyanani,nisingeremba kudadeki.Mkubalie mtoto yule.Unaniangusha bratha”
“Achana naye”
“Alafu Monalisa yule vipi?Mbona anakushobokea sana”
“Monalisa yupi?”
“Yule Form four Z!”
“Demu wake Amir?”
“Demu wake waaapi?Sio demu wake wala nini,basi anashobo huyooo”
Abraham na Lazaro walizungumza siku hiyo na Lazaro alikuwa akimchambua kila msichana wa shule hiyo na kumueleza Abraham jinsi anavyosifiwa,kabla hajafika mbali Mwalimu Beatrice akatokea kwa mbele na kupunga mkono.
“Mimi?"
Lazaro akaitikia huku akajinyooshea yeye kidole!
“No,Abraham”
Abraham,akachukuwa barua na kuiweka mfukoni kisha kutembea mpaka kwa Mwalimu Beatrice.
“Bado hujaondoka Abraham?”
Lilikuwa ni swali ambalo jibu lake lilikuwa wazi kwani Abraham alikuwa katika mazingira ya shule bado.
“Bado Mwalimu”
“Una subiri nini sasa?”
“Nilikuwa namalizia home work ya Civics”
“Aya,embu naomba unisaidie haya madaftari kunipelekea nyumbani kwangu”
Mwalimu Beatrice,alikuwa ni mdogo wa umbo mzuri wa sura!Kwa haraka haraka ungemuangalia ungedhani wenda ni mwanafunzi wa chuo kikuu.Lakini alikuwa ni mwalimu wa shule hiyo ya Msingi Makuburi,katika walimu wa kike waliokuwa wanaongoza kwa kutongozwa ofisini ni mwalimu huyu Beatrice sababu alikuwa ni mzuri,mbali na uzuri wake alikuwa mwenye umbo lililobinuka kidogo kwa nyuma.Hiyo ilifanya kiuno chake chembamba kijichore sawa sawia.Shepu yake ilifanya mpaka walimu wenzake wampachike jina la Utani na kumuita kiuno dondora!Walimu karibia wote walishindwa kumpata, kifupi alikuwa ndege mjanja lakini alinasa kwenye tundu bovu,Abraham alitokea kuizuzua akili yake.Kwa maana hiyo kwa taaluma yake na utu uzima, kazi hiyo ilikuwa ni ndogo sana ingawa ilikuwa ni aibu nzito kama mfano angekutwa ana mahusiano na mwanafunzi wake,ingekuwa ni skendo kubwa shuleni.Alijuwa anafanya makosa lakini alitaka kuufuata moyo wake unataka nini.Ndiyo maana akatumia gia ya kumpa Madaftari Abraham ili waongozane mpaka kwenye kota wanazoishi walimu,nyuma ya shule.
“Abraham”
Mwalimu Beatrice akageuka na kumuita Abraham kwani yeye alikuwa anaongoza mbele,Abraham nyuma.
“Naam mwalimu”
“Unaishi wapi?”
“Kawe”
“Kawe ipi?”
“Pale Kawe Mwisho,ukishuka unaingia ndani ndani kidogo”
“Kwahiyo kila siku unatokea Kawe?”
“Ndio Mwalimu”
“Napenda sana ulivyo smart”
Haukuwa utani,katika wanafunzi waliokuwa wanaongoza kwa Usafi ni Abraham,hata siku moja Abraham hakuwahi kuwasili shule akiwa hajapiga pasi nguo zake,mkanda nje,tai shingoni.Hiyo ilimfanya azidi kuonekana maridadi na uzuri wake ukaongezeka zaidi na zaidi!
“Ahsante Mwalimu”
“Nani huwa anakupasia nguo zako?”
“Mimi mwenyewe”
“Nice”(Vizuri)
Mwalimu Beatrice alizidi kumwaga sifa huku akijitahidi kumzoea Abraham na kuyasoma mawazo yake,walivyofika nyuma ya shule wakatembea hatua nyingine kumi na kuufikia mlango uliokuwa na geti kwa nje yaani grili,Mwalimu Beatrice akatoa funguo kutoka mfuko wa Sketi yake,akafungua geti na mlango!
“Karibu ndani Abraham”
“Hapana Mwalimu,nawahi nyumbani”
“No,ingia.Usijali.Vua viatu hapo,leta nikupokee madaftari”
Bado Abraham hakuelewa niya na madhumuni ya mwalimu wake,isingekuwa jambo heshima asingekubali kuingia ndani kwani Mvulana huyu hakuwa mtu wa kujirahisisha na kuyumbishwa katika misimamo yake,kwa kuwa alimchukulia kama mwalimu wake,akakubali na kuingia ndani.
Ambapo alikumbana na Seble ndogo,yenye makochi matatu!Moja kubwa na mengine madogo madogo!
“Unakunywa soda gani?”
Mwalimu Beatrice akaanza kuchombeza!
“Hapana mwalimu nina haraka”
“Abraham,inaelekea una wasiwasi sana eeh.Embu acha uwoga,au nikuletee pombe?”
“No no,pombe sinywi”
“Subiri basi hapo”
Mwalimu Beatrice,akaingia chumbani kwake lakini alihisi jasho linamtoka na wakati huohuo damu yake inamwenda mbio,kitu alichotaka kwenda kukifanya kwa mwanafunzi wake alikiogopa na hakujua ni wapi aanzie na mfano ingetokea Abraham angekataa sijui angeiweka wapi sura yake ingekuwa ni aibu ya mwaka, kwa maana hiyo ili kuzuia aibu hiyo ilikuwa ni lazima jambo lake litimie.
Vitu hivyo vilipita kichwani kwake akiwa anatoa nguo moja baada ya nyingine!Alivyohakikisha hana nguo hata moja alichukuwa kitenge,akakizungusha mwilini mwake,akachukuwa na kingine na kukifunga kifuani.
Akatembea mpaka kwenye friji ambalo lilikuwa humohumo chumbani kwake,akachukuwa soda ya sprite!
“Mimi ni mwanamke,huyu ni mtoto mdogo kwangu.Yupo kwenye balehee.Hawezi kutoka”
Mwalimu Beatrice aliwaza kichwani huku akitoa soda,akapita seblen na kummiminia Abraham ndani ya glasi.
“Usijali kuhusu haya mavazi,kuna joto sana.Karibu Soda”
“Nakunywa haraka haraka niwahi nyumbani Mwalimu”
Abraham alivyomaliza kuongea sentensi hiyo akaweka glasi mdomoni bila kuishusha, akamaliza yote,akamimina tena akaiweka mdomoni akawa kama mtu mwenye kiu kali anayekunywa maji ya kunywa, hakuelewa kwa kufanya hivyo alikuwa akimkera sana Mwalimu huyu wa Biology,aliyekuwa na mikakati mingi sana kichwani kwake ya kufanya naye ngono siku hiyo.
“Aya Mwalimu Ahsante sana.Nawahi nyumbani sijafanya homework ya Mwalimu Ndubusa”
“Fanyia hapahapa tu”
“Acha tu niende mwalimu”
Kila njama aliyotaka kutumia Mwalimu Beatrice aliona kama inagonga mwamba,alichofanya ni kutembea mpaka mlangoni na kufunga mlango kwa ufunguo akarudi kwa Abraham,ilikuwa ni lazima ajitose kimaso maso kwani asingeweza kulala bila kufanya uzinzi na mwanafunzi wake Abraham,ndiyo maana akamsogelea Abraham karibu kabisa!
“Abraham”
Mwalimu Beatrice aliita huku akimshika Kidevu Abraham,jambo lililomfanya mtoto huyu aanze kuogopa!
“Mbona unaogopa?Ushawahi kufanya?”
“Kukukukuku kufanya nini Mwalimu?”
“Kufanya mapenzi”
“Hapana”
“Subiri nikuoneshe kitu”
Wakati Mwalimu Beatrice anaongea maneno hayo mkono wake ulikuwa unapita taratibu kwenye kaptula ya Abraham,akafika mpaka juu ya zipu yake.
“Mmmmh”
Mguno huo ulitoka kwa Mwalimu Beatrice baada ya kugusa karoti ya Abraham,ukubwa wa Karoti hiyo ulimshangaza zaidi.Hiyo ilimfanya Abraham aanze kuogopa zaidi na zaidi ingawa hata yeye alihisi mwili wake unabadilika,damu inamwenda kasi.Mwalimu huyu hakuishia hapo,alifungua zipu ya Abraham na kutoa karoti ambayo ilikuwa tayari imesimama dede na misuli ilikuwa pembeni imekaza.Unene na urefu wa karoti ya Abraham ulimfanya Mwalimu Beatrice,atumbue macho yake kwani hakutegemea kama mtoto huyu mdogo angekuwa na mtalimbo mkubwa namna hiyo.Bila kuuliza kitu kingine zaidi akafungua mdomo wake, akajaza mate mengi juu ya ulimi na kuitumbukiza karoti ya Abraham kinywani.
Kwa mara ya kwanza Abraham alihisi kama amepigwa na shoti ya umeme mwilini.Hakuelewa, ni kitu gani kilitokea lakini ndani ya dakika mbili alifungua macho yake na kujikuta yupo uchi wa mnyama juu ya kochi la Mwalimu wake,alipigwa na butwaa la waziwazi lakini akili yake haikuwa hapo hata kidogo.Vitu vyote aliviona lakini hakuweza kujigusa hata kidogo,alimuona sana Mwalimu Beatrice ametoa nguo zake zote,na yupo juu yake analazimisha karoti iingie ndani ya mgodi wake.Abraham alikuwa kama amepararaizi mwili mzima, hasa ndizi yake ilivyoingia ndani ya mgodi,joto alilohisi lenye ladha ya kipekee haikuwa ya kawaida!Akabaki anatoa macho yake kama mjusi aliyebanwa na mlango.
“Abra..ham nishike hapa”
Mwalimu Beatrice alisema huku akiichukua mikono ya Abraham akaiweka kiunoni mwake, akachukuwa tena mikono ya Abraham akaweka juu ya maziwa,Mwalimu Beatrice akawa kama dereva siku hiyo sababu mchezo mzima alikuwa anauendesha mwenyewe.Hiyo ndiyo ilikuwa mara ya kwanza kwa Abraham kuona chachandu ya mwanamke na kufanya mapenzi.Utamu aliokuwa akihisi wakati Mwalimu Beatrice ananyonga kiuno, ilimfanya aanze kufumba macho yake,kuna vitu alianza kuhisi vinatembea ndani ya mwili wake kuanzia miguuni mpaka mgongoni.Na kadri sekunde zilivyozidi kwenda mbele ndipo alipozidi kuhisi rahaa!
“Aa aah aah sshs”
Huyu alikuwa ni mwalimu Beatrice akiwa juu ya kiuno cha Abraham,bahati mbaya ilikuwa kwake kwani alihisi tayari Abraham amemwaga mate ndani ya mgodi wake,hakuweza kumuachia kwani hata yeye alikuwa karibu ukingoni.Akazidi kujisugua kwa nguvu mpaka alipoachia pumzi nzito,akatulia.Sekunde ishirini baadaye ndipo akili ya Abraham ikawa imekaa sawa,akakurupuka na kumtoa mwalimu huyu pembeni!
“Mwalimu!Kwanini umefanya hivi?”
“Abraham bas…”
“Nini?Umefanya nini?Ujuwe wewe ni mwalimu wangu”
“Abraham subiri basi kwanza”
“Siwezi kusubiri.Nipe nguo zangu”
Abraham alivyoona anacheleweshwa aliinua nguo zake kutoka chini na kuziweka mwilini kabla ya kuvaa akaanza kutembea kuelekea mlangoni,alivyonyonga kitasa akakuta mlango umefungwa.
“Fungua mlango”
Ilikuwa ni kauli iliyoambatana na ukali.
Mwalimu Beatrice hakuwa na sababu ya kuendelea kubishana,akaokota kanga yake na kuchukuwa funguo,kabla ya kuufikia mlango alisikia mtu anagonga kwa nje!
“Ngo! Ngoo! Ngooo!”
Hali hiyo ilimfanya asite kidogo.
“Naniiii?”
Akauliza.
“Fungua mlango Bite”
Mapigo ya moyo ya Beatrice yalipiga kwa nguvu kama kitenesi na kugonga kifua chake kwani sauti iliyotokea nje ya mlango aliijua fika ni ya Mchumba wake Mwanajeshi, Luteni Shadrack Mwalusambo!Alivyomuangalia Abraham akahisi kama kinyesi kinataka kumpenya.


Mwalimu Beatrice alihaha waziwazi,sauti ya Mchumba wake ilimchanganya akashindwa ni kitu gani akifanye, hiyo ilifanya hata Abraham aliyekuwa kando yake apigwe na bumbuazi,japokuwa hakuelewa ni nani aliyekuwa nje anabisha hodi lakini alielewa ndiyo aliyemfanya Mwalimu wake asite kufungua mlango.Kufungua mlango kwa wakati huo na Abraham kuonekana hana shati mwilini ingeleta picha mbaya na wenda ingepelekea matatizo mengine zaidi kwani Mwalimu Beatrice alimfahamu fika Mchumba wake jinsi alivyokuwa mwenye wivu na mkorofi endapo akiona vitu visivyoeleweka,hilo ndilo lilizidi kumvuruga ubongo kwa kiasi cha kutosha.
“Abraham vaa shati njoo huku”
Mwalimu akaropoka huku akimvuta Abraham mpaka seblen.
“Vaa haraka”
Kwa jinsi alivyokuwa anaongea kwa kunong’ona ilimfanya Abraham azidi kutandwa na hofu.
“Kwani kuna nini?”
“Vaa shati kaa hapo”
Akakimbia haraka chumbani kwake na kuvaa blauzi na sketi,akafuta majasho yake,akanyoosha moja kwa moja mpaka mlangoni na kufungua.
“Mbona umechelewa kunifungulia?”
Mwalimu Beatrice alikumbana na swali hilo.
“Nilikuwa chumbani.Karibu ndani”
“Ahsante”
Luteni Shadrack alikuwa ni mrefu kwenda hewani,kifua chake kilikuwa kikubwa,mweusi,ana misuli mpaka usoni ilionekana alikuwa ni mwenye nguvu na mtu wa mazoezi mno,alivyoingia mpaka seblen alikumbana na Abraham juu ya kochi.
“Hujambo dogo?”
“Sijambo shikamoo”
Abraham aliitikia huku akitupa macho yake juu ya dafatri aliloweka kwa ajili ya kuzuga!
“Wewe Bite,huyu mwanafunzi anafanya nini hapa?”
“Ni mwanafunzi wangu”
“Mwanafunzi si huko shuleni.Kwani hapa ni shule?”
“Hapana Darling aliniomba nije kumuelekeza homew..”
“Mbona mlango ulikuwa umefungwa?”
Kabla ya Mwalimu Beatrice kumaliza kujibu kile, alidakwa na swali lingine.Hiyo ilimfanya azidi kutetemeka na kutafsiri kwamba wenda Mchumba wake tayari amechezwa na machale.
“Huwa sipendi kuacha mlango wazi,naogopa.Kitu chochote kinaweza kuingia Darling”
Mwalimu Beateice alijitetea lakini jibu lake halikujitosheleza kabisa kwani Mwanajeshi huyu alizidi kumkandamiza maswali.
“Jina lako nani dogo?”
Swali hilo lilimdondokea Abraham,akahisi kama uti wake wa mgongo umepulizwa na ubaridi mkali.
“Abraham”
“Mbona unajifanya mjanja sana.Jina lako nani?”
Luteni Shadrack akauliza,tena kwa ukali kidogo huku akitoa bastola yake kiunoni,akaiweka mezani.Hiyo ilimfanya Abraham ahisi kama mkojo unataka kumpenya,aliitizama bastola kwa hofu kubwa na jasho la kwapa lilianza kumtoka.
“Naitwa Abraham”
“Unapoulizwa jina lako inabidi utaje majina yako yote matatu.Nyie watoto wa siku hizi mnakuaje”
“Abraham Deo Karekezi”
“Namna hiyo.Siku nyingine ukiulizwa jina unatakiwa kujibu namna hiyo”
“Upo kidato cha ngapi?”
“Cha tatu”
“Unaishi wapi?”
“Kawe”
“Hapa unafanya nini?”
“Alikuja nimfundishe Biology”
Mwalimu Beatrice akadakia sababu aliona tayari maji ya shingo!Na alimuona Abraham anavyotetemeka kwa hofu.
“Sasa mbona daftari lenyewe limegeuzwa?”
Hilo lilikuwa swali lingine kutoka kwa mwanajeshi ambaye hakuwa ana onesha sura ya kucheka hata kidogo,maswali hayo aliuliza kwa ukauzu.
“Nilikuwa nimesimama upande wa huku.Baby muache mtoto wa watu kwanza akapumzike kwao,maana hapo nakujuwa wewe kwa maswali”
Mwalimu Beatrice akaongea huku akijichekesha kidogo ili kuuwa soo!
“Lazima nimchangamshe kidogo.Mtoto wa kiume siku zote lazima uwe sharp”
“Sasa huyu mtoto wa watu hajui mambo ya jeshi.Abraham nenda nyumbani tutaonana kesho darasani.Make sure unaenda kupitia pitia tena”
Hiyo ndiyo gia aliyotumia mwalimu huyu Beatrice kumtoa Abraham kwenye mdomo wa mamba.
Bila kugeuka nyuma, Abraham alisimama na kuzoa madaftari yake mezani na kuyaweka ndani ya begi,akanyoosha mpaka mlangoni na kutokomea bila kugeuza shingo kwani alihofia wenda angesimamishwa tena,wakati anatembea njiani aliapia hatorudi tena nyumba za kota nyumbani kwa Mwalimu Beatrice.
Muda ulikuwa umekwenda na tayari kigiza cha usoni kilikuwa kimeingia,alichofanya ni kutembea mpaka stendi ya mabasi ‘External’ hapo alisubiri gari la Mwenge kwa dakika karibia arobaini na tano nzima ndipo alipopata daladala ingawa lilikuwa limejaa,akasimama na kushika bomba huku akitafakari kichwani namna ambavyo alivyokuwa nyumbani kwa mwalimu Beatrice wanafanya tendo hilo la kuzini.Bado picha,akiwa chini mwalimu wake juu iliendelea kumpitia kichwani akawa kama anajitizama kwenye kioo,ilikuwa ndio mara yake ya kwanza kufanya tendo hilo,tena na mwalimu wake, alihisi kujuta lakini kwa upande mwingine alihisi yeye ni mshindi kwani alisikia marafiki zake wakipiga stori jinsi wanavyofanya ngono na wasichana,alitabasamu na kushuka Mwenge mwisho ambapo hapo alichukuwa daladala lingine la Kawe!
Kitendo cha kufika tu,alipitiliza moja kwa moja mpaka chumbani kwake,akabwaga begi na kunyoosha bafuni ambapo huko alijimwagia maji.
“Mwalimu Beatrice”
Akiwa bafuni maji yakiwa yanammwagikia alisema huku akishika kombola lake na kuliangalia,bado hakuamini pia alikuwa ameona nguo ya ndani ya mwalimu wake.Mwalimu huyo ambaye alisikia chini ya kapeti kwamba anasumbua sana kwa uzuri.
“Sasa mimi mbona kaja mwenyewe.Ah kesho nitamuadithia Lazaro.Kumbe haya mambo matamu sana”
Abraham alizidi kutafakari!
*********
Hata ilivyokuwa kwa Mwalimu Beatrice,baada ya mchumba wake kuondoka usiku wa saa tano,alibaki akimfikiria na kumuwaza Abraham kichwani namna ambavyo Mashine ya mwanafunzi huyo ilivyoingia mpaka ukingoni,ukubwa wa Mashine ya Abraham ndiyo ilimfanya atafakari zaidi na zaidi,picha ya jinsi alivyokuwa juu ya kochi,amemlalia Abraham juu yake iliendelea kumsumbua kichwani.Akatamani muda urudi nyuma ili aendelee kulisakata rumba,kifupi siku hiyo kichwa chake kilitawala Abraham na wala sio kitu kingine chochote kile.
Siku hiyo baada ya kujimwagia maji na kuandaa ‘topic’ atakazofundisha kesho yake, alienda seblen na kuangalia kochi walilokuwa wanafanyia mapenzi na Abraham,bado alikumbuka.
Picha ya Abraham ilimjia kichwani na alitamani kukuche akaonane naye shuleni,kabla ya kutembea hatua mbili chini aliona karatasi ndogo yenye mistari mekundu kwa juu.Akaiokota na kuifungua,ulikuwa ni mwandiko wa kike na chini kulikuwa na michoro mingi ya kopa,hapo hapo akapandisha macho yake juu ili aanze kuisoma.
‘Kwako kipenzi cha roho yangu Abraham,ni siku nyingi sana nilikuwa nikikuambia juu ya hisia zangu lakini naona kama hunielewi, unanipotezea.Naomba nikwambie kwamba nakupenda sana nipo tayari kufa kwa ajili yako.Wewe ni barafu wa moyo wangu.Kama gari wewe mafuta,siwezi bila wewe Abraham.Nishagombana na rafiki yangu Diana kisa wewe.Nachokuomba unikubalie.Ukifanya hivyo nitakupa zawadi nzuri sana.Naomba unijibu hii barua utakapoipata please.Wako kipenzi,Veronica Deniss!’
Hayo ndiyo maandishi yaliyosomeka juu ya karatasi aliyokuwa anasoma Mwalimu Beatrice,alihisi kuumia moyo kabisa,wivu ulimjaa!Akachukuwa barua hiyo na kuikunja kunja vizuri.
“Hili swala lazima nilipeleke kwa mkuu wa shule.Lazima Vero aondoke kwenye shule”
Hivyo ndivyo alivyoapia Mwalimu huyu Beatrice,hakukuwa na sababu yoyote ya kumtimua mwanafunzi huyo aliyeitwa Veronica Denis lakini kutokana na wivu ilimbidi afanye hivyo,hakuwa tayari kumuona Abraham anatembea na mtu yoyote Yule na swala hilo akalifumbia macho.
Siku hiyo, usingizi kilikuwa ni kitu hadimu sana kupatikana.Saa kumi na moja kamili juu ya alama, alitoka kitandani na kuanza kupiga pasi nguo alizochagua kuvaa,akaweka vitabu na madaftari sawa tayari kwa kuingia shuleni,akazama bafuni kuoga.
Mawazo yake yote yalikuwa kwa Veronica Denis na tayari ndani ya masaa machache alitokea kumchukia vibaya sana,ilivyotimu saa kumi na mbili kasoro, akaanza safari ya kwenda shuleni,ambapo huko alikuta wanafunzi wapo mstarini, wanashika namba,alivyoangalia vizuri mstarini alimuona Abraham.Namba zikachukuliwa harakaharaka lakini Veronica hakuonekana bado,kumaanisha kwamba alikuwa amechelewa namba na hilo ndilo alilotaka litokee apate pa kuanzia.
Katika wanafunzi wote wa shule ya sekondari Makuburi Abraham ndiye aliyeonekana kinara,sio kwa utanashati ama uzuri kote alitisha, hiyo ilimfanya ajichotee umaarufu,jina lake lilizungumziwa kila pembe ya kona.Ilikuwa ni lazima ukikuta genge la wasichana watatu ama wawili ni lazima jina la Abraham litatajwa tu, hilo lilifanya mpaka wanafunzi wa kidato cha juu yake waanze kumfuatilia,hata baadhi ya walimu ilikuwa hivyohivyo pia.Sio siri mtoto huyu alikuwa homa ya shule,alitokea kutingisha shule nzima, jina lake likavuma kwa kasi kama kimbunga!
“Leo tunaenda kuangalia topiki ya Aljebra,Jana nilifundisha Exponent ingawa sikueleweka vizuri.What is Aljebra?”
Madam Monica Sikwese, alikuwa ubaoni siku hiyo, anafundisha hesabu na huyu ndiye alikuwa mwalimu wa zamu wiki hiyo.
Alikuwa ni madam anayeogopeka pengine na karibia nusu shule kwani alikuwa ni mkali kuliko pilipili mbuzi,hakuwa ana mchezo linapokuja swala la kufundisha, ndiyo maana wanafunzi wengi walimuogopa na walianza kutetemeka sababu alikuwa ana tabia ya kuchagua mtu yoyote ajibu swali.
“Rose Msuya,what is Aljebra?”
Madam Monica aliuliza huku akiwa ameshikilia fimbo yake sawasawa kabisa mkononi,tayari kwa kutembeza mikwaju darasani.
“Aljebra is..Aljebra is the study of science that deals with a….”
“Go Infront”(Nenda mbele)
Hiyo ilimaanisha kwamba Rose Msuya, akasubiri adhabu ya fimbo kwani tayari alikuwa ameingia chaka,nyuma yake alikuwa amekaa Abraham hata yeye alionekana kutokujiamini sababu somo la hisabati kwake lilikuwa ni ugonjwa mkubwa sana.
“What is your name again?”(Jina lako nani tena)
Madam Monica alimtupia swali Abraham,alionekana kama amelisahau jina lake kidogo.
“Abraham Karekezi”
“Okay,What is Aljebra young boy?”
“Mwalimu mimi sijui”
Hapohapo Abraham alipigwa fimbo ya mgongo,ikamuingia akajikunja.Kabla ya kukaa sawa akapokea nyingine.
“What is Aljebra?”
Madam huyu aliuliza swali huku akizidi kumshushia Abraham fimbo za mgongo,haikuleweka kama alikuwa ana bifu nae ama la.Kwani aliendelea kumchalaza fimbo,maumivu aliyohisi Abraham hakuweza kuyavumilia, hapohapo akasimama na kuishika fimbo ya mwalimu huyu anayemchapa hovyohovyo..
“Wewe unataka kufanya nini?”
Bila kujibu chochote Abraham akavunja vunja fimbo kwa hasira.
“Mwalimu huwezi kunipiga hivyooo”
“Huna adabu,njoo hapa.Mpumbavu,njoo ofisini”
Jambo hilo liliwashangaza sana wanafunzi waliokuwa darasani, hakuna hata mmoja aliyeweza kuamini macho yake kwamba Abraham angefanya jambo kama hilo.
“Njoo ofisini”
Madam Monica alimkwida shati Abraham na kumvuta.
“Usinishike hivyo basi ticha za wapi hizo”
Abraham alikuwa tayari keshavimba kama chura wa masika,hasira zimempanda, macho yamebadilika rangi yakawa mekundu kama mtu aliyevuta bangi.
“Niachie, usinishike hivyo basi,naenda mwenyewe ofisini.Lazaro nipe begi langu,huyu ticha kavu sana”
Abraham alikasirika kiasi kwamba hata rafiki yake Lazaro, alimwogopa kwani tangu aanze kumjua Abraham hakuwahi kumuona akiwa katika hali kama hiyo,hilo liliwafanya wanafunzi wote wabaki midomo wazi.
“Safi sana jembe,ungempiga vitasa huyo choko”
Hiyo ilikuwa sauti ya kukwaruza kutoka kwa mwanafunzi mwingine kutoka kiti cha nyuma, ilielekea hata yeye alimchukia sana Madam Monica!
Abraham na Madam Monica wakaongozana mpaka ofisi ya mwalimu mkuu,moja kwa moja Madam Monica akaanza kuelezea jinsi ilivyokuwa.
“Piga magoti kwanza hapo,piga magoti nimesema”
Mwalimu mkuu aliyefahamika kwa jina la Abdallah Henku, alisema kwa ukali kwani jambo hilo lilimkera kwa kiasi cha kutosha.Abraham akapiga magoti huku akisubiri hukumu kwani alijuwa tayari huo ndio ungekuwa mwisho wa masomo yake katika shule hiyo.
“Nashangaa akashika fimbo,akaivunja…”
Madam Monica akamalizia kutoa unoko wake!Mlango wa ofisini ukagongwa,akaingia Mwalimu Beatrice,kitendo cha kumuona Abraham yupo chini kapiga magoti, kilimuuma sana,akataka kujuwa ni kitu gani kafanya.



Kitu kilichomfanya Mwalimu Beatrice aingie ofisi ya mwalimu mkuu ilikuwa ni kumchongea Veronica Denis,ilikuwa ni lazima ampatie barua ya mapenzi iliyoandikwa na msichana huyo, akimtaka kimapenzi Abraham lakini picha aliyoikuta ilimfanya asitishe zoezi lake kwanza,ilikuwa ni lazima ajuwe ni kitu gani Abraham kipenzi cha roho yake, amefanya nini.
“Abraham umefanya nini?”
Mwalimu Beatrice alijikuta ameuliza bila kutarajia,kwa namna ambavyo roho ilimuuma alitamani amwambie Abraham, asimame lakini hakuwa na mamlaka hayo hata kidogo.
“Mimi sijui kosa langu”
Abraham akajibu huku akitizama chini,kwa tukio alilofanya alijua kusimamishwa shule ni halali yake.
“Hujui kosa lako?”
Madam Monica, akadakia akiwa amevimba kwa hasira.
“Ndio sijui kosa langu ticha”
“Kosa lako ni utovu wa nidhamu na dharau na jambo hili,hatuwezi kulifumbia macho ni lazima usimamishwe shule”
“Poa tu”
Abraham alijibu kwa kiburi, kutokana na hasira alizokuwa nazo, hiyo ilifanya mwalimu Beatrice amkingie kifua,kufukuzwa kwa Abraham shuleni hapo ingemgharimu sana.
“Abraham kwanini unakuwa mtovu wa nidhamu?Mwalimu naomba niachie mimi huyu mtoto”
“Ongea na mwanafunzi wako”
Mwalimu Mkuu nayeye akatoa neno.
“Huyu hawezi kubaki kwenye hii shule”
Madam Monica akakaza uzi, hakutaka kuendelea kumuona Abraham shuleni hapo,niya yake alitaka asimamishwe ama afukuzwe shule kabisa.
“Hapana Madam Monica,hili swala umelifikisha ofisini.Niachie mimi nitajua cha kufanya”
Mwalimu Mkuu aliyefahamika kwa jina la Sir.Abdallah Henku alihitimisha na hilo ndilo lililofanyika kwani Madam Monica aliondoka huku nyuma akisisitiza kwamba Abraham hatakiwi shuleni hapo.
“Kwanini unakuwa mtovu wa nidhamu?”
Mwalimu Mkuu akamtupia swali Abraham,Mwalimu Beatrice nayeye alikuwa pembeni anasikiliza atakachojibu Abraham.
“Alikuwa akinichapa hovyohovyo.Sikuweza kuvumilia Sir”
“Ilikuwaje?”
Abraham akaanza kuelezea jinsi ilivyokuwa mpaka mwisho.
“Sir.Henku naomba usimfukuze huyu mtoto,ni mwanafunzi wangu”
“Lazima aadhibiwe kwanza ndiyo mengine tutajua”
Mwalimu Beatrice aliendelea kusisitiza kwamba Abraham asamehewe, ikiwezekana apewe hata adhabu lakini sio kufukuzwa shule.
Hivyo ndivyo ilivyokuwa, Abraham aliponea kwenye tundu la sindano kwani mwalimu mkuu aliagiza kengele ya dharura igongwe ili wanafunzi wakusanyike mstarini.
“Jesca,nenda kwa mwalimu Juma mwambie aje na fimbo.Mwite na Sir.Kipwate na Madam Monica”
Walimu wote waliotajwa hapo walikuwa wakali mno,ilikuwa wazi kwamba siku hiyo Abraham anaenda kushambuliwa kama mwizi kwa viboko na adhabu juu.
Wanafunzi walianza kutoka madarasani baada ya kusikia kengele ya dharura imegongwa,ilikuwa ni lazima wakusanyike mstarini hata kama walikuwa na vipindi.
Dakika kumi na tano baadaye,walikuwa mstarini nje ya uwanja mkubwa wapo kimnya na mwalimu mmoja mmoja alianza kujongea.Hakuna hata mwanafunzi mmoja aliyejuwa nini kinataka kutokea lakini kuna baadhi walizipata habari,chini ya kapeti kwamba Abraham ndiye anafukuzwa shule siku hiyo, baada ya kumdindia Madam Monica.
“Ndio hivyo,jamaa alishika fimbo akavunja kudadeki.Mimi sikujua kama Abraham mtata namna ile.Macho yake yalikuwa mekundu Mamaee mpaka nikaogopa”
Hiyo ilikuwa minong’ono katikati ya gwaride.
“Kamdindia Madam Monica?”
“Khaaa!Kidogo wapigane unaambiwa,Madam Monica kamshika shati,Abraham kapangua Mamaae”
“Wee!Abraham huyu Karekezi?Form Three?Nawewe tukana taratibu basi, humuoni Sir.Lang’o?Huwezi kuongea mpaka kutukana”
“Ndio, Mamaeee”
“Maskini.My Handsome,kwahiyo atafukuzwa?”
“Sijui sasa”
Jinsi fimbo zilivyokuwa nyingi mbele ya mstari ambapo walisimama walimu iliogopesha,kila mtu alianza kumuonea huruma Abraham, mwanafunzi aliyekuwa anatingisha kwa uzuri na utanashati.
Abraham hakuwa mwenye wasiwasi hata kidogo kwani alipanga agome tena kuchapwa mbele ya kadamnasi, isipokuwa Mwalimu Beatrice alimsihii sana na kumuomba.
“Abraham kubali uchapwe My Love,yaishe leoleo”
Mwalimu Beatrice alimbembeleza afanye hivyo na kujaribu kumpetipeti wakiwa wenyewe ofisi ya mwalimu Mkuu.
“Hapana Mwalimu,siwezi kuchapwa nakwambia”
“Please baby,nakupenda Abraham”
“Kwahiyo kama unanipenda ndio niumie?Mimi sio Yesu,niumie kwa ajili yako”
“Sijasema hivyo Abraham wangu,nakupenda kubali kuchapwa”
“Nishasema hapana siwezi”
“Abraham”
Mwalimu Beatrice alizidi kuumia moyo na machozi yalianza kumlenga,alifanya kila analoweza ili kuzituliza hasira za Abraham lakini jitihada zake ziligonga mwamba,hazikuzaa matunda.Hiyo ilizidi kumuumiza zaidi mtima, pengine aliwaza labda Abraham hakuelewa nini maana ya mapenzi.
“Nakupenda Abraham”
Hapohapo mlango wa ofisini ulifunguliwa, akaingia mwalimu Mkuu, Sir.Abdallah Henku.
“Njoo huku”
Hapo ndipo Mwalimu Beatrice akazidi kuchanganyikiwa zaidi,alijuwa tayari mwisho wa kumuona Abraham umefika,akamuangalia kwa masikitiko makubwa mno.
“Nenda kapige magoti pale mbele”
Abraham akatembea,umbali wa mita tano ndipo kulikuwa na uwanja mkubwa ambapo aliwaona wanafunzi wenzake wamesimama mstarini,akapiga picha jinsi atakavyoenda kuchapwa viboko mbele ya alaiki ya wanafunzi wenzake.
Ndani ya moyo wake kulikuwa na nafsi mbili moja ilikuwa laini ikimwambia kuwa akubali siku moja yaishe na nyingine ilimwambia adinde, asikubali kuchapwa kama mbwai iwe mbwai,bado alitembea huku akitafakari.Ghafla sura ya Baba yake mlezi Mr.Chonga ilimjia kichwani kwake jinsi alivyokuwa mtata,kufukuzwa kwake shule ingepelekea kupokea kipondo kingine endapo akifika nyumbani,hiyo ilimfanya atafakari tena upya.
“Piga magoti hapo”
Madam Monica akamdaka kwa ukali akiwa ameshika fimbo ndefu,Abraham akatii amri na kupiga magoti chini huku akiwatizama wanafunzi wenzake waliokuwa kimnya wanamuangalia,alishangaa namna ambavyo shule ilivyokuwa kimya sana na yenye uzuni.
“Good afternoon everyone…i just want to tell you one thing today....Let me use swahili.Unajuwa hakuna kitu kibaya hapa duniani kama dharau.Mwalimu akikuchapa siku zote anakupenda na wala hakuchukii,sisi ni kama wazazi wenu.Lakini nashangaa wengi wenu mnakuwa viburi.Mfano mdogo,huyu Abraham mimi sikutegemea hata siku moja kama ana tabia alizoonesha leo kwa mwalimu Monica.Swala hilo sitolifumbia macho hata kidogo, Never.Kwahiyo huyu atakuwa wa mfano.Mwalimu Kishamba nipatie kiboko”
Sir.Henku alimaliza kuzungumza na kukabidhiwa fimbo akamsogelea Abraham.
“Go down,Kiss the floor”

*******
ENDELEA KUSOMA HADITHI NA SIMULIZI ZA MTUNZI….EMMANUEL F.KWAY(THE STORY MASTER)

156 comments:

  1. Магазин спортивного питания, официальный сайт которого доступен по адресу: SportsNutrition-24.Com, реализует обширный выбор товаров, которые принесут пользу и заслуги как профессиональным спортсменам, так и любителям. Интернет-магазин осуществляет свою деятельность уже многие годы, предоставляя клиентам со всей России качественное спортивное питание, а также витамины и специальные препараты - https://sportsnutrition-24.com/nochnye-vosstanoviteli/. Спортпит представляет собой категорию продуктов, которая призвана не только сделать лучше спортивные заслуги, но и положительно влияет на здоровье организма. Схожее питание вводится в повседневный рацион с целью получения микро- и макроэлементов, витаминов, аминокислот и белков, а также других недостающих веществ. Не секрет, что организм спортсмена в процессе наращивания мышечной массы и адаптации к повышенным нагрузкам, остро нуждается в должном количестве полезных веществ. При этом, даже правильное питание и употребление растительной, а также животной пищи - не гарантирует того, что организм получил необходимые аминокислоты или белки. Чего нельзя сказать о качественном питании для спорта. Об наборе товаров Интернет-магазин "SportsNutrition-24.Com" реализует качественную продукцию, которая прошла ряд проверок и получила сертификаты качества. Посетив магазин, заказчики могут найти себе товары из следующих категорий: - L-карнитинг (Л-карнитин) представляет собой вещество, схожее витамину B, синтез которого осуществляется в организме; - гейнеры, представляющие из себя, белково-углеводные консистенции; - BCAA - средства, содержащие в собственном составе три важнейшие аминокислоты, стимулирующие рост мышечной массы; - протеин - чистый белок, употреблять который можно в виде коктейлей; - современные аминокислоты; - а также ряд прочих товаров (нитробустеры, жиросжигатели, особые препараты, хондропротекторы, бустеры гормона роста, тестобустеры и все остальное). Об оплате и доставке Интернет-магазин "SportsNutrition-24.Com" предлагает огромное обилие товаров, которое полностью способно удовлетворить профессиональных и начинающих атлетов, включая любителей. Большой опыт дозволил фирмы наладить связь с наикрупнейшими поставщиками и изготовителями питания для спорта, что позволило сделать политику цен гибкой, а цены - демократичными! К примеру, аминокислоты или гейнер приобрести можно по цене, которая на 10-20% ниже, чем у конкурентов. Оплата возможна как наличным, так и безналичным расчетом. Магазин предлагает обширный выбор методов оплаты, включая оплату разными электронными платежными системами, а также дебетовыми и кредитными картами. Главный кабинет фирмы размещен в Санкт-Петербурге, но доставка товаров осуществляется во все населенные пункты РФ. Помимо самовывоза, получить товар вы можете с помощью любой транспортной фирмы, подобрать которую каждый клиент может в личном порядке.

    ReplyDelete
  2. Гадание на дам на картах значится максимально достоверным вариантом определить судьбу человека. Погодные проявления или церемониальные жертвоприношения с течением времени основали конкретное объяснение обнаруженного. Изначальные варианты хиромантии образовались тысячи лет назад до Н.Э.

    ReplyDelete
  3. Используя бесчисленную переадресацию ни один человек не может выследить клиента. Заходите в сеть форума гидра обход Иланский лишь в режиме невидимки. Допускается применить для верификации на форуме ГидраРУ инновационный протокол TOR. Многоканальное зашифрование гарантирует отличную величину защищенности для всех пользователей портала HydraRU.

    ReplyDelete
  4. Крупнейший инетрнет-сайт гидра зеркало onion – ваш актуальный ассистент при борьбе с сетевыми нападениями. Преступники реализуют незаконную деятельность по разнообразнейшим поводам. По большей части хакеры атакуют клиентов с целью материальной выгоды. В мире IT технологий как никогда просто стать целью взломщиков.

    ReplyDelete
  5. Гарантировать иммунитет сличения возможно исключительно на специальной платформе https://onion.hydraruzxpnew4afx.com. Не на каждом шагу нужно прописывать индивидуальные данные, прийдется лишь только отыскать удобную платежную систему. Наиболее известные платежные системы требуют стопроцентной идентификации пользователей.

    ReplyDelete
  6. Магазин Hydra распространяет уникальные товары по всей территории бывшего союза. Всем покупателям сайта гидра через тор браузер 2022 предлагается широкий выбор вещей, которые нельзя найти в стандартном маркете. Проект обладает множеством положительных достоинств, среди каких надо отметить достойный уровень сохранности выполненных контрактов.

    ReplyDelete
  7. На странице hydraclubbioknikokex7njhwuahc2l67lfiz7z36md2jvopda7nchid гидра зеркало официальный hydparu zerkalo site вы сможете обнаружить гаджеты на персональный вкус и сумму. Магазин функционирует на протяжении пяти лет, и за этот период умудрился проявить себя как лучшая торговая площадка. UnionГИДРА – это крупнейший интернет-магазин, где возможно приобрести необходимые продукты по максимально хорошей стоимости. В настоящий момент 99 процентов всех коммерческих операций осуществляют в инете.

    ReplyDelete
  8. Перспективная платформа hydraclubbioknikokex7njhwuahc2l67lfiz7z36md2jvopda7nchid как перевести на гидру позволяет получить необходимый товар немедленно. Анонимные операции в сети интернет считаются приоритетом для каждого онлайн-магазина. Не включая защиты при покупках посетители на каждом шагу думают спрятать информацию о себе.

    ReplyDelete
  9. Перевести денежные средства нужному человеку или конкретной компании запросто любыми методами. Самый естественный метод незамеченного оплаты электронных счетов – это отыскать данные на http://rahgoddess.co.uk/entry/the-project-begins-1-4.html. В настоящее время представлено большое число цифровых кошельков.

    ReplyDelete
  10. Приобрести незаметность есть возможность исключительно на индивидуальной платформе http://www.elbache.de/wb/pages/gaestebuch.php. Не в каждой платежной системе необходимо прописывать личные данные, достаточно лишь использовать положительную систему платежей. Непосредственно старые виртуальные кошельки потребуют необходимой проверки пользователя.

    ReplyDelete
  11. Обще бытовое применение листов прочного и легкообрабатываемого материала вполне велико. Фанеру влагостойкую лист фанеры влагостойкой применяют не исключительно в кораблестроении. При выпуске шкафов или внутренней декорации комнат, для производства уникальных вещей декора, для покрытия бортов грузовых машин - это только неполный перечень применения общепринятого водоустойчивого материала.

    ReplyDelete
  12. Стоит только зарегистрироваться на странице HydraRU, а пользовательская информация направится для хранения в кодированном формате на виртуальном серваке. С помощью сервиса https://hydraclubbioknikokex7njhwuahc2l67lfiz7z36md2jvopda7nchid.onion-f.com юзеры обретут высокую степень скрытности. Сайт HydraRU обеспечит каждому посетителю высочайший уровень анонимности при обработке всякой сделки.

    ReplyDelete
  13. Всякая сделка на http://renebiemans.nl/users.php?m=details&id=15563 обеспечивает посетителям высокую степень анонимности. Множество юзеров догадываются о сайте Гидра, тем не менее зайти в него довольно тяжело. Безликая покупка осуществляется именно в сети даркнета. Человеку нет необходимости подвергать самого себя опасности, осуществляя покупку у поставщика продукта.

    ReplyDelete
  14. Всевозможные комплектующие и даже программный код необходимо оформлять дистанционно. Присутствует востребованная продукция, выкупить какую имеется возможность лишь через сеть. На сайте http://www.pc28lt.com/space-uid-205171.html выставлен громадный ассортимент продуктов на любой вкус. Нынешний человек закупает абсолютно значительное количество продуктов удаленно.

    ReplyDelete
  15. Инновационный интернет-магазин совершает специализированную работу на протяжении последних 6 лет и как и прежде энергично совершенствуется. Доставка продуктов из Hydra осуществляется по всей РФ. Огромное число грамотных поставщиков http://fujiapuerbbs.com/home.php?mod=space&uid=2460963 обеспечат отличный товар по минимальному курсу. На форуме Гидра найдется громадное число товаров любого назначения.

    ReplyDelete
  16. С целью проплаты продуктов в маркете ГидраUnion используют виртуальные кошельки, либо криптографию. Покупателю нет необходимости самолично общаться с продавцом, любую закупку допустимо оплачивать онлайн. Формирование криптоиндустрии дает перспективу всем юзерам проекта https://hydraclubbioknikokex7njhwuahc2l67lfiz7z36md2jvopda7nchid.onion-o.com устраивать персональные покупки на всяком расстоянии.

    ReplyDelete
  17. Лучший игровой ресурс по реализации досуга в сети интернет – Гидра http://fjclwz.us/upload/home.php?mod=space&uid=195723

    ReplyDelete
  18. Самой популярной причиной для выставления анонимного платежа http://iraneyeresearch.com/index.php?subaction=userinfo&user=avobafari считается подработка в мировой сети. К тому де придется указывать, что скрытные покупки проводят не исключительно злоумышленники, но и обычные юзеры. Заплатить за покупку скрытно стает довольно сложно. Представьте, ведь ни один человек не решится заплатить существенные деньги как налоги без всякого, оформляя качественную аферу.

    ReplyDelete
  19. Наш веб-сайт рассказывает о новостях бокса и ММА. Читатель узнает о ближайших и прошедших боях - рейтинг ufc. Эксперты делятся своими прогнозами на наиблежайшие действия, проводят разбор окончившихся поединков. Можно прочитать интервью со знаменитыми бойцами и их тренерами. Новости ММА, бокса Все предстоящие и прошедшие бои освещаются с подробным разбором, анализом и комментариями спортивных экспертов. Подписавшись на Octagon, вы будете в курсе всех событий в области боевых искусств. Самые интересные, запоминающиеся бои без правил в нашем видеоконтенте. Ознакомьтесь с выводами, разбором захватывающих моментов поединков. Действия, расписание, видео На странице указано расписание грядущих боев. Даты, время начала боя вы можете изучить на портале. Предлагается просмотр видео самых увлекательных моментов схваток. Кто не желает заниматься скучным чтением, может посмотреть видео прогноз. Легкая, юмористическая подача информации очень просто воспринимается и усваивается у подписчиков. Видеоряд постоянно обновляется, предлагается только высококачественный контент. Биографии, рейтинги боксеров Предоставлены полные биографии знаменитостей, рейтинг UFC. Вы узнаете, каким был путь героя к покорению Олимпа. Приводятся все весовые характеристики атлетов. Предоставляется информация о самочувствии боксера до и после поединка. Проводится разборка стиля и техники бойцов. Octagon.express предлагает только полностью достоверную информацию. На нашем интернет-сайте вы ознакомитесь и узнаете о всех тонкостях смешанных боевых искусств. Точные прогнозы, достоверные рейтинги - наше основное кредо. Подписавшись на Telegram канал, вы будете в курсе всех новостей боевых искусств. Все последние бои UFC не ускользнут от вас.

    ReplyDelete
  20. Hydra – объективный просветительский портал http://www.bigapple.idv.tw/discuz/home.php?mod=space&uid=1472269

    ReplyDelete
  21. Наш онлайн-кинотеатр предлагает своим зрителям погрузиться в мир интересных турецких сериалов. Портал предлагает широкий каталог многосерийных фильмов на любой вкус, а главное, все они имеют русское озвучивание. Мы регулярно пополняем медиатеку, чтобы нашему гостю не приходилось находить новинки на сторонних ресурсах - турецкие сериалы бесплатно. Что предлагает онлайн-кинотеатр своим посетителям? - Полное отсутствие рекламы. Ничего не сможет отвлечь от игры любимых актеров! - Постоянные обновления каталога. Теперь вы не пропустите новинки турецкого кинематографа! - Качественное озвучивание - долой русско-турецкий словарь! - Возможность смотреть сериалы на различных устройствах. Дорога на работу теперь станет увлекательной и интересной! - Удобство просмотра. Наш видеопроигрыватель может остановить только низкая скорость интернет-соединения. Портал турецких сериалов создан специально для тех, кто всегда находится в поиске ресурсов, позволяющих смотреть иностранные многосерийные фильмы без ограничений. Сейчас в вашем распоряжении огромное количество кинофильмов с отличным качеством изображения и русским переводом. Начать просмотр можно любому посетителю онлайн-сайта без каких-то ограничений. Но мы все таки советуем вам пройти минутную регистрацию - это позволит вам создавать закладки, оставлять комменты и обсуждать просмотренные картины с другими пользователями портала. А в случае если вы только начали знакомство с турецкими сериалами, сделать выбор в пользу той или иной фильмы поможет короткая аннотация. Погрузится в мир головокружительной любви, трагических встреч, кровопролитной вражды и опасных игр с самой судьбой поможет наш онлайн-кинотеатр сериалов из Турции. Позитивного просмотра и положительных эмоций!

    ReplyDelete
  22. Ставки на спорт с каждым днем становятся все популярнее. У беттеров (игроков на ставках) из Узбекистана появилась возможность делать ставки в национальной валюте на сайте - получить бонусы БК Mostbet в Узбекистане. При регистрации в этой букмекерской конторе пользователь выбирает игровую валюту - узбекский сум, русский рубль, доллар либо евро. Всего доступно 19 валют! Играть на веб-сайте сумеют не только жители Узбекистана, ресурс переведен на 25 языков. Ставки на спорт На сайте Мостбет можно сделать ставки на все главные события мира спорта - футбол, баскетбол, хоккей, волейбол, теннис и другие, включая зимние виды спорта, легкую атлетику и единоборства. Для того, что бы делать ставки надо пройти функцию регистрации, которая займет не более 5 минут. Для клиентов этой букмекерской конторы доступны ставки до матча (прематч) и в режиме реального времени (Live). Казино В Мостбет можно так же сыграть в азартные игры - карты, рулетку и слоты (игровые автоматы с вращающимися барабанами). Слотов очень много - на любой вкус, от традиционных вишенок-клубничек до современного софта с несколькими игровыми полями и бонусными раундами. На Мостбет у игроков единый счет для ставок и для казино. Приложение на сайте Мостбет можно загрузить приложение для игры с мобильных устройств - планшетов и смартфонов под управлением операционной системы Андроид и iOS. Ссылка для скачивания этих программ располагается в самом верху главной страницы. На веб-сайте можно ознакомиться с отзывами игроков. В случае если имеется проблема со входом на портал, то на странице «Зеркало» вы можете выяснить об альтернативных методах входа, в случаях блокировки ресурса. Для связи с пользователями действует онлайн чат, в котором вы можете задать любой интересующий вопрос техническим консультантам букмекерской конторы.

    ReplyDelete
  23. Портал Mostbethit.net предлагает посетителям поближе познакомиться с одноименной БК. Интернет-ресурс посвящен описанию основных преимуществ конторы. На проекте пользователи узнают другие важные моменты - получить бонусы Мостбет. Букмекерская контора для продвижения зеркальных ссылок использует партнерские сайты. Одним из таких ресурсов стал описываемый проект. На страничках портала посетители найдут: - ссылки на зеркала букмекера; - описание БК; - правила работы с конторой; - особенности бонусной политики; - действующие промокоды; - описание способов пополнения баланса; - анализ отзывов о букмекере; - рекомендации для создания аккаунта. Проект предлагает детальный «разбор» оператора ставок. Регистрация для использования не нужна. Гость может свободно переходить по разделам, получать информацию. Языковая доступность - плюс онлайн-сайта. Русская версия раскрывается по умолчанию. Пользователь может установить любой из 23 доступных языков. Описания на портале детальные. Создатели попытались отметить каждый аспект. Для улучшения пользовательского восприятия тексты снабжены снимками экрана. Информативность максимальная. Предложенные на проекте ссылки направят игроков на действующее зеркало БК. Это обеспечивает круглосуточный доступ к конторе. Об использовании VPN и многих других способов обхода санкций Роскомнадзора удается забыть. Ссылки на дублирующий интернет-сайт Мостбет предложены на каждой странице. Долго находить действующие адреса не придется. Разработчики выпустили мобильную версию онлайн-сайта. Проект оптимизирован под девайсы с разной диагональю дисплея. Пользоваться ресурсом удобно со смартфонов и планшетов. Интернет-портал не предлагает спортивных ставок и других азартных утех. Закрыть веб-сайт регулятор не может. В итоге ресурс обеспечивает круглосуточный доступ к БК.

    ReplyDelete
  24. Кибербезопасность отныне считается собственным видом для обеспечения приятной работы в сети. Только лишь достаточный уровень понимания дает вам протекцию частных данных. Например, hydra рабочий 2022 делится конкретными указаниями, чтобы не стать заложником киберпреступников в интернете.

    ReplyDelete
  25. Интернет-сайт Mostbethit.net предлагает посетителям ближе познакомиться с одноименной БК. Интернет-ресурс посвящен описанию главных преимуществ конторы. На проекте пользователи узнают другие принципиально важные моменты - Мостбет. Букмекерская контора для продвижения зеркальных ссылок использует партнерские веб-сайты. Одним из таких ресурсов стал описываемый проект. На страничках портала пользователи увидят: - ссылки на зеркала букмекера; - описание БК; - правила работы с конторой; - особенности бонусной политики; - действующие промокоды; - описание способов пополнения баланса; - анализ отзывов о букмекере; - консультации для создания аккаунта. Проект предлагает детализированный «разбор» оператора ставок. Регистрация для использования не нужна. Посетитель может свободно переходить по разделам, получать информацию. Языковая доступность - плюс интернет-сайта. Русская версия открывается по умолчанию. Пользователь может установить любой из 23 доступных языков. Описания на портале детальные. Разработчики попытались отметить каждый нюанс. Для улучшения пользовательского восприятия тексты снабжены снимками экрана. Информативность максимальная. Предложенные на проекте ссылки направят игроков на действующее зеркало БК. Это обеспечивает круглосуточный доступ к конторе. Об использовании VPN и прочих способов обхода санкций Роскомнадзора удается забыть. Ссылки на дублирующий веб-сайт Мостбет предложены на каждой странице. Долго находить действующие адреса не придется. Разработчики выпустили мобильную версию интернет-сайта. Проект оптимизирован под девайсы с разной диагональю дисплея. Пользоваться ресурсом комфортно со смартфонов и планшетов. Портал не предлагает спортивных ставок и других азартных утех. Закрыть сайт регулятор не может. В результате ресурс обеспечивает круглосуточный доступ к БК.

    ReplyDelete
  26. В последние годы популярность зарубежных телесериалов и полнометражных фильмов бьет все рейтинги. Но где их можно посмотреть? В интернете много онлайн-кинотеатров, которые предлагают просмотр интересных киноработ от иностранных кинокомпаний - турецкие сериалы на русском. Большой выбор на любой вкус Но в особенности комфортно смотреть зарубежные киносериалы и фильмы на интернет-сайте Turksezon.net. На этой платформе представлена огромная подборка самых популярных сегодня фильмов. На площадке вы можете бесплатно смотреть различные проекты: - турецкие; - колумбийские; - индийские; - бразильские. Все зарубежные проекты на площадке идут на российском языке. Привлекательно не только лишь отличное качество перевода, да и высочайшее разрешение. Многие сериалы и полнометражное кино на портале идут в формате 720 HD. Широкое разнообразие зарубежных фильмов - одна из особенностей онлайн-кинотеатра. На интернет-сайте представлены сериалы и полнометражное кино в самых различных жанрах. Тут обязательно найдутся достойные внимания проекты для ценителей драм, фэнтези, боевиков, комедий. Имеется огромное количество криминальных, исторических, семейных и военных киноработ. В соответствующих рубриках собраны популярные детективы, триллеры, мелодрамы. Фантастическое кино, в том числе сериалы, можно получить в отдельном блоке. Такое ранжирование по жанрам очень удобно для выбора подходящего кинофильма. Удобство поиска увлекательных фильмов Еще одна особенность онлайн-кинотеатра заключается в удобстве поиска интересного фильма. Каждый гость может найти кино, которое выпущено в определенный период. На веб-сайте в отдельных блоках располагаются проекты, выпущенные с 2016 до 2022 годы соответственно. К каждому кинофильму на площадке идет маленькое, но емкое описание. Благодаря ему каждый гость сможет найти именно тот проект, что ему максимально интересен.

    ReplyDelete
  27. Retivabet - наиболее перспективный и простой букмекерский интернет-сайт - ставки на спорт. На интернет-сайте вы можете получить разнообразные виды развлечений на любой вкус: казино, букмекерские ставки, игры. Если вы любитель казино, здесь для вас предусмотрено все необходимое. Легкий доступ к игровым слотам, карточным играм и рулетке, а помимо этого возможность поучаствовать в турнире. Главная задача турнира - вырваться на лидирующие позиции в турнирной таблице, потому что крупный призовой фонд будет разделен между первыми тридцатью победителями. И чем выше ваша позиция в таблице, тем больший кусок пирога вам достанется. Для ценителей спорта Retivabet предлагает обширный спектр ставок. Здесь находятся не только всемирно известные чемпионаты и команды, но и новички из разных лиг и стран, что делает результат еще более волнительным и интересным. Футбол, баскетбол, хоккей, теннис, снукер, дартс, скачки, гонки и многое другое, на чем можно заработать хорошие деньги. Выбор за вами. Киберспорт кроме этого стал неотъемлемой частью букмекерской компании. Теперь клиент может делать ставки не только на Пре-Матчи, но и на игры в режиме онлайн, в любое время дня и ночи. Для того, чтобы стать клиентом огромной семьи Revitabet, нужно пройти регистрацию на интернет-сайте Retivabet.net. Это не займет более десяти минут, после чего новый клиент получает бонусы от организации, которыми в последствие, может пользоваться на свое усмотрение. Виды бонусов: - Приветственные; - Кешбэк с сумы ставок; - Бонус за серию проигрышей; - Экспресс бонус. Пополнение счета возможно разными вариантами, что делает это максимально удобным для клиентов. Можно использовать для пополнения и вывода денежных средств банковские карты, мобильные платежи, интернет банкинг. Никаких комиссий со стороны букмекерской компании, и даже приятные бонусы за пополнения. Никаких подводных камней, только прозрачно чистое и выгодное развлечение!

    ReplyDelete
  28. Веб-сайт казино Супер Слотс представляет собой хорошее сочетание удобства и функционала. Любой из разделов обустроен опциями, которые будут понятны и полезны любому гостю - регистрация Super Slots. Сайт предлагает пройти несложную и быструю регистрацию. Это можно сделать 3-мя способами: при помощи аккаунта в социальных сетях, номера телефона или электронной почты. После регистрации открывается кошелек для пополнения средств и весь ассортимент слотов. Говоря о доступных слотах, стоит отметить богатую коллекцию онлайн-сайта. Она нередко обновляется и включает в себя как классические слоты, так и новинки игровой индустрии с необычными правилами. Количество слотов на портале превосходит 200 штук. Также на сайте показан сегмент с широкой линейкой призов. К ним относятся депозитные и бездепозитные бонусы. Депозитные отличаются разнообразными предложениям в форматах приветствия, кэшбека, турниров и розыгрышей. Бездепозитные призы находятся фриспинами, которые игроки получают благодаря промокодам. Промокоды, в свою очередь, это бесплатное вознаграждение от сайта. Они даются бесплатно как новым, так и старым игрокам. Их раздача связана с особенными датами, открытием новейших слотов либо крупными турнирами. С помощью промокодов гости получают все виды бонусов, представленные на сайте. Более того, портал предлагает установить официальное приложение. В соответствующем разделе можно изучить мобильную версию, не уступающую в функционале компьютерной. Стоит упомянуть, что для обеих версий идиентично качественно работает служба поддержки. Сайт казино информативен и грамотно спроектирован. Он предлагает большое количество функций и услуг, которые вы можете без труда получить в несколько кликов. Тут каждый игрок становится счастливым пользователем.

    ReplyDelete
  29. В последние годы известность зарубежных сериалов и полнометражных фильмов бьет все рейтинги. Но где их вы можете посмотреть? В интернете немало онлайн-кинотеатров, которые предлагают просмотр интересных киноработ от зарубежных кинокомпаний - турецкие фильмы. Огромный выбор на любой вкус Но в особенности удобно смотреть зарубежные сериалы и фильмы на веб-сайте Turksezon.net. На этой платформе представлена большая подборка самых популярных сегодня фильмов. На площадке вы можете бесплатно смотреть различные проекты: - турецкие; - колумбийские; - индийские; - бразильские. Все зарубежные проекты на площадке идут на российском языке. Привлекательно не только отличное качество перевода, но и высокое разрешение. Многие киносериалы и полнометражное кино на веб-сайте идут в формате 720 HD. Обширное обилие зарубежных кинофильмов - одна из особенностей онлайн-кинотеатра. На сайте находятся сериалы и полнометражное кино в самых разных жанрах. Здесь непременно найдутся интересные проекты для ценителей драм, фэнтези, боевиков, комедий. Есть огромное количество криминальных, исторических, семейных и военных киноработ. В соответствующих рубриках расположены востребованные детективы, триллеры, мелодрамы. Фантастическое кино, в том числе сериалы, вы можете найти в отдельном блоке. Такое ранжирование по жанрам очень удобно для выбора подходящего фильма. Удобство поиска увлекательных фильмов Еще одна особенность онлайн-кинотеатра заключается в удобстве поиска интересного фильма. Каждый гость может подобрать кино, которое выпущено в определенный период. На сайте в отдельных блоках расположены проекты, выпущенные с 2016 до 2022 годы соответственно. К каждому фильму на площадке идет маленькое, но вместительное описание. Благодаря ему каждый гость сумеет найти именно тот проект, что ему наиболее интересен.

    ReplyDelete
  30. Высочайшая степень безопасности при сделке на ГидраРУ http://www.thedesidossier.com/2014/02/nigar-current-loves-january.html

    ReplyDelete
  31. Если вы думаете, что покупать потребные продукты по удобной ставке есть возможность лишь на сайтах крупных торговых площадок, то сильно ошибаетесь. Забирайте товары всего лишь у проверенных продавцов на форуме Hydra. Сайт hydraclubbioknikokex7njhwuahc2l67lfiz7z36md2jvopda7nchid гидра анион зеркало предоставляет личным пользователям поистине серьезный запас нужных продуктов по максимально приемлемым ценам.

    ReplyDelete
  32. Целый ряд грамотных продавцов отпускают свои товары в любой регион РФ. Проверить честность маркета реально по отзывам на страницах http://hfren.com/home.php?mod=space&uid=140338. Для формирования договора клиенту следует зарегистрироваться на главном портале. Верифицироваться на портале Гидра возможно с использованием любого гаджета, или ноута.

    ReplyDelete
  33. Подключение прокси так же является абсолютным вариантом авторизации гидра через зеркало для организации нужных покупок. Личные сведения клиента автоматически содержатся на центральном дата-центре Hidra. ВПН позволяет сделать невидимым прямой адрес владельца, гарантируя надежную скрытность закупки веществ.

    ReplyDelete
  34. Вообразите, все же ни один человек не захочет заплатить дополнительные денежки как налог за глаза, оформив качественную аферу. Более того, стоит учитывать, что персональные поступления проводят не только хакеры, но и обыкновенные пользователи. Особо частым фактором для выставления скрытого счета hydraclubbioknikokex7njhwuahc2l67lfiz7z36md2jvopda7nchid официальный сайт гидры онион считается работа в сети интернет. Оплатить покупки незамеченным стало очень сложно.

    ReplyDelete
  35. Вдобавок возможно использовать инкогнито при заходе на портал Hydra. Зарегистрироваться на https://onion.hydraruzxpnew4afc.com элементарно через уникальный браузер TOR. Для моментального коннекта с главным сервером проекта требуется хороший VPN. Мультиканальная переадресация позволит авторизироваться на портале моментально и безопасно.

    ReplyDelete
  36. Реально ли залогиниться на портал крупного интернет-магазина Hydra невидимкой http://607080hj.net/space-uid-4021.html

    ReplyDelete
  37. Ссылки для входа на проект UnionГИДРА довольно часто изменяются. Посетителям маркета представлены тысячи реализаторов с всякими товарами. Немыслимый состав веществ старая гидра совершенно поражает воображение. Проводите лишь защищенные виды проплаты веществ. С целью идентификации на площадке Гидра нужно применять дополнительную ссылку стартовой страницы Hidra.

    ReplyDelete
  38. К работе приглашаются водители с собственным высокотаннажным автотранспортом. Просмотрев страницу перевозчика по юрл грузоперевозки недорого без посредников, каждый пользователь может глянуть виды оказываемых услуг.

    ReplyDelete
  39. Стоит заметить, что скамейку для дачи недорого в москве купить считается особым типом уличной мебели. Лучший вид отдыха на участке дачи – воспользоваться стальной скамьей в тени вашего палисадника. Чугунные части конструкции гарантируют очень большой срок применения скамеечки. Лавки для дачного участка производятся из деревянного полотна на стальной основе.

    ReplyDelete
  40. На портале МедСпрос функциональные детские медицинские кровати по самой хорошей цене от поставщиков. Фирма МедСпрос числится крупным продавцом медицинского оборудования. Современные кровати рассчитаны для расположения больных, которым требуется все время быть в положении лежа.

    ReplyDelete
  41. Все выставленное оборудование прошло испытания и отличается высоким качеством. Мед кровати, чаще всего, потребуются обследуемым с нарушением опорно-двигательного аппарата, или пожилым людям. На платформе реализатора MED СПРОС общебольничные медицинские кровати представлен широкий перечень особой врачебной техники.

    ReplyDelete
  42. Характеристики любой развлекательной конструкции сможет занять малышей на продолжительный период. Малышу станет очень интересно прокатиться на качели, а также залезать по конструктивным деталям. Показанные на сайте SunnyToyRU комплекты игровой домик для улицы имеют уникальный внешний вид.

    ReplyDelete
  43. Фирма SunnyToyRU предоставляет всем родителям http://weloveokinawa.com/home/userinfo.php?uid=3672 по преимущественно доступной стоимости от производителя. Ребенок не сможет просто просиживать на лавочке без энергичных игр. Для осуществления развлечений девочек и мальчиков используются игровые комплексы для детей. Фундаментальные сооружения обеспечат безопасность ребенка при играх.

    ReplyDelete
  44. Нынешнее искусство будь то картина картины маслом на холсте купить нацелено добавлять серьезного разнообразия в серые будни. Яркий постер станет радовать глаз всегда, если только надоест – совсем быстро заменить, оформив заказ на новый экземпляр. Высокой уважением в последнее время имеют постеры из знаменитых или сегодняшних кинопроизведений. Портреты то и дело оформляют в раме, а плакаты просто размещают на стене.

    ReplyDelete
  45. Дети постарше будут иметь возможность повышать основные навыки. Малыши не переставая будут исследовать игровую площадку для детей. На площадке расставят все нужные конструктивы – горка, качели, лестница. Комплекс http://mkutepliydom.ru/forums/user/ovowylaz/ сумеет целиком принять все интересы подростков в развлечениях.

    ReplyDelete
  46. Мечты по теме приготовления еды очень легко проделать за счет набора для кухни Dream Toys. В небольшом наборе для кухни найдутся все подходящие для досуга компоненты. Отличный вариант игровая кухня понравится малышам младшего возраста. Небольшой кухонный набор предоставит шанс девочке самостоятельно исполнять ежедневные операции родителей, которые они видят.

    ReplyDelete
  47. Большой ассортимент плакатов и точные репродукции картин на сайте ДасАрт постеры в стиле лофт

    ReplyDelete
  48. Достойным подбором для самых маленьких станет http://linguage.cn/home.php?mod=space&uid=53159 компании Дрим Тойз. Отличное сырье и гипоаллергенная обшивка – гарантия здоровья ребенка. Подбирайте современные лошадки-качалки только в официальных маркетплейсах Санни Той. Игрушка подойдет на текущий вес и возраст малышей.

    ReplyDelete
  49. Любая девчонка представляет себя маленькой модницей. Полноразмерный детский набор в полной мере имитирует реальный туалетный столик. Для наведения мейкапа девчонкам нужен http://www.liuwenzheng.com.cn/home.php?mod=space&uid=833817&do=profile. Нужный объем украшений элементарно распределить в детском туалетном столике Дрим Тойз.

    ReplyDelete
  50. Все опубликованные на страницах Gamer Plus игры разделяются по конкретным стилям. Стоит перейти gamer-plus, и посетитель постоянно будет в курсе последних новшеств интерактивной области. В целях определенного понимания уместности вышедших игр нужно использовать рейтинг.

    ReplyDelete
  51. Проверенный партнер в области создания сайтов http://l50763ns.bget.ru/index.php?subaction=userinfo&user=irozukip

    ReplyDelete
  52. Большинство пользователей Инстаграма хотели бы увеличить количество фолловеров, просмотров, комментариев и лайков. Самым быстрым способом может стать накрутка за деньги, конкретно такие услуги предлагают на интернет-сайте Krutiminst.ru - накрутка подписчиков на инстаграм

    ReplyDelete
  53. Влагостойкая фанера ФСФ - сфера использования http://www.ztbaxh.com/member/index.php?uid=epycobyp

    ReplyDelete
  54. Vanessa Williams (43 лучших фото) подборка https://cojo.ru/

    ReplyDelete
  55. Стрижки для пожилых людей (38 лучших фото) UHD https://cojo.ru/pricheski-i-strizhki/strizhki-dlya-pozhilyh-lyudey-38-foto/

    ReplyDelete
  56. Лорел Лэнс - 39 лучших фото подборка cojo.ru

    ReplyDelete
  57. Осипов Юрий (44 лучших фото) милые картинки https://cojo.ru/znamenitosti/osipov-yuriy-44-foto/

    ReplyDelete
  58. Удлиненное каре без челки на тонкие волосы крутые фото https://cojo.ru/pricheski-i-strizhki/udlinennoe-kare-bez-chelki-na-tonkie-volosy-34-foto/

    ReplyDelete
  59. Малек форели лучшие картинки https://cojo.ru/zhivotnye/malek-foreli-44-foto/

    ReplyDelete
  60. Девушки с чёрными волосами в хорошем качестве https://cojo.ru/devushki/devushki-s-chyornymi-volosami-70-foto/

    ReplyDelete
  61. Лазарев Анатолий Телеведущий крутые фото https://cojo.ru/znamenitosti/lazarev-anatoliy-televeduschiy-50-foto/

    ReplyDelete
  62. Открытка с днем рождения, бабочки, цветы крутые фото https://cojo.ru/pozdravleniya/otkrytka-s-dnem-rozhdeniya-babochki-tsvety-19-foto/

    ReplyDelete
  63. Картинки коньяк лучшие картинки https://cojo.ru/kartinki/kartinki-konyak-61-foto/

    ReplyDelete
  64. Деревенский натюрморт классные фото https://cojo.ru/izobrazitelnoe-iskusstvo/derevenskiy-natyurmort-53-foto/

    ReplyDelete
  65. Грустный фон аниме классные фото https://cojo.ru/fony/grustnyy-fon-anime-57-foto/

    ReplyDelete
  66. Деревенский натюрморт смотреть фото https://cojo.ru/izobrazitelnoe-iskusstvo/derevenskiy-natyurmort-53-foto/

    ReplyDelete
  67. 3D Fire Tiger Wallpapers WallpapersHigh.com hd fast and free https://wallpapershigh.com/3d-fire-tiger

    ReplyDelete
  68. High Resolution Avatar The Last Airbender Wallpapers WallpapersHigh.com FullHD absolutely free https://wallpapershigh.com/high-resolution-avatar-the-last-airbender-wallpapers

    ReplyDelete
  69. Army Special Wallpapers wallpapershigh.com High Res absolutely free https://wallpapershigh.com/army-special

    ReplyDelete
  70. Aesthetic Sun And Moon Wallpapers WallpapersHigh.com high res absolutely free https://wallpapershigh.com/aesthetic-sun-and-moon

    ReplyDelete
  71. Hanuman Chalisa Wallpapers WallpapersHigh.com high resolution 100% free https://wallpapershigh.com/hanuman-chalisa

    ReplyDelete
  72. Avengers Infinity War Wallpapers wallpapershigh.com High Resolution 100% free https://wallpapershigh.com/avengers-infinity-war

    ReplyDelete
  73. Amazing Space Wallpapers wallpapershigh.com HIGH QUALITY 100% free https://wallpapershigh.com/amazing-space

    ReplyDelete
  74. High Definition Marbl wallpapershigh.com Fullhd for free https://wallpapershigh.com/high-definition-marbl

    ReplyDelete
  75. Aesthetic Balloon Wallpapers wallpapershigh.com high definition for free https://wallpapershigh.com/aesthetic-balloon

    ReplyDelete
  76. House Painting Wallpapers Wallpapershigh.com https://wallpapershigh.com/house-painting

    ReplyDelete
  77. Streamer Tati Wallpapers https://wallpapershigh.com https://wallpapershigh.com/streamer-tati

    ReplyDelete
  78. Buggy One Piece Wallpapers wallpapershigh.com https://wallpapershigh.com/buggy-one-piece

    ReplyDelete
  79. Law Enforcement Police Wallpapers https://wallpapershigh.com https://wallpapershigh.com/law-enforcement-police

    ReplyDelete
  80. Your car might be stolen if you don't keep this in mind!

    Imagine that your car was taken! When you visit the police, they inquire about a specific "VIN lookup"

    Describe a VIN decoder.

    Similar to a passport, the "VIN decoder" allows you to find out the date of the car's birth and the identity of its "parent" (manufacturing facility). You can also find out:

    1.Type of engine

    2.Model of a car

    3.The limitations of the DMV

    4.The number of drivers in this vehicle

    You'll be able to locate the car, and keeping in mind the code ensures your safety. The code can be viewed in the online database. The VIN is situated on various parts of the car to make it harder for thieves to steal, such as the first person seated on the floor, the frame (often in trucks and SUVs), the spar, and other areas.

    What happens if the VIN is intentionally harmed?

    There are numerous circumstances that can result in VIN damage, but failing to have one will have unpleasant repercussions because it is illegal to intentionally harm a VIN in order to avoid going to jail or the police. You could receive a fine of up to 80,000 rubles and spend two years in jail. You might be stopped by an instructor on the road.

    Conclusion.

    The VIN decoder may help to save your car from theft. But where can you check the car reality? This is why we exist– VIN decoders!

    ReplyDelete
  81. ДВП https://fanwood.by/v-klimovichakh/shop/dsp-dvp-i-mdf считается без преувеличения используемым облицовочным материалом в строительной сфере. Есть огромное количество типов влагостойкой фанеры, одной из которых является ламинированная ФОФ. Покрытая с одной или нескольких сторон тонкой пленкой, фанера способна наиболее полно противостоять неблагоприятным погодным условиям.

    ReplyDelete
  82. Фанерная плита ФСФ - это влагостойкий вид фанеры, получивший крупное распределение в строительстве. Как водится смоляно фенолформальдегидную фанеру https://fanwood.by/ применяют как поверхностный облицовочный материал. Для внутренних действий применять смоляно фенолформальдегидную плиту невозможно - будут испаряться вредные субстанции при конкретных условиях. Влагонепроницаемый вид практически не вбирает жидкость, а по окончании высыхания возвращается к своей первоначальной форме.

    ReplyDelete
  83. А14 Бионикл – современный микропроцессор в схеме мобильных устройств на данное время. Четырнадцатый Айфон укомплектован многофункциональным микропроцессором A14 Бионикл https://www.iport.ru/products/productID118890/, что является самым инновационным микропроцессором в индустрии. Передовая методика предлагает модернизированную продуктивность отклика с программами и браузером.

    ReplyDelete
  84. Дизайн, в том числе яркий дисплей https://meiying99.com/home.php?mod=space&uid=382118

    ReplyDelete
  85. Внешний вид, вдобавок крутой дисплей айфон 14 про макс esim темно-фиолетовый 1024 гб

    ReplyDelete
  86. Теперь езачем оплачивать подписку и тратить денежки на просмотр мультфильмов в онлайне. 100 000 сериалов в российском переводе предоставлены посетителям сервиса «Кино Навигатор» именно бесплатно. Действительно элементарный способ смотреть http://m-squash.ru/index.php?subaction=userinfo&user=nonstopmogul63 после работы – это посетить кинотеатр «Кино Навигатор».

    ReplyDelete
  87. С той целью, чтобы получить возможность управлять погрузчиком, нужно пройти специальное обучение и успешно сдать экзамены, свидетельствующие знания в данной области. Водительское удостоверение тракториста-машиниста предоставляется в Гостехнадзоре и в обязательном порядке для тех, кто задумывает трудиться на специальной технике - права на погрузчик

    ReplyDelete
  88. Пневмогидравлический узел постоянно используется в машиностроении. Важные компоненты гидравлики https://pneumo-center.by/shop/1730---klapan-otsechnoy1946/ зачастую возможно найти в большой строительной технике, так например, трактор. Большинство аграрной техники работает на гидравлике, так например, сеть полива, так же прочая техника для сельского хозяйства.

    ReplyDelete
  89. Гидро компонент применяют с целью контроля расходом необходимой жидкости в гидросистемах. С целью хорошей работы механизмов в системе гидравлики устанавливается муфта упругая кулачковая купить. Данные системы считаются важным компонентом пневмогидравлических компонентов и используется в определенных сферах производства.

    ReplyDelete
  90. Дженнифер Лопес 32 лучших фото смотреть фото https://cojo.ru/

    ReplyDelete
  91. Бонусы и поощрений в БК 1хбет существенно повышает привлекательность компании в глазах пользователей. Очень выгодные предложения доступны как новеньким, и пользователям, уже имеющим опыт работы на платформе. Среди впечатляющего ассортимента бонусной программы очень очень просто потеряться. Каждый промокод 1хбет обеспечит право на определенные преференции - действующий промокод 1xbet.

    ReplyDelete
  92. БК MelBet пользуется большой известностью на российском рынке: -Деятельность компании лицензирована; - Пользователям предоставлен внушительный список ставок - в формате live и предматчевых; - Тут нет задержек с выплатами. Линия ставок неописуемо презентабельна. Для того, чтобы получить выгодный бонус на совершение ставок, нужно всего лишь использовать промокод MelBet RS777. Получить промокод вы можете на ставку либо на депозит. Каждое предложение имеет свои особенности отыгрыша - MelBet промокод при регистрации на сегодня.

    ReplyDelete
  93. В 2023 году промокод 1хбет предоставляющий наибольший бонус - 1XFREE777. Бонусные средства начисляются автоматически на отдельный счет и их сразу же вы можете использовать для игры - бесплатный промокод 1xbet на сегодня.

    ReplyDelete
  94. Заказать продукцию предприятия Samsung в сети брендовых онлайн магазинов телефоны samsung galaxy s Пермь - значит купить первоклассное и устойчивое устройство, то которое станет вашим любимым, безупречным ассистентом в домашних условиях. Мы безостановочно расширяем ассортимент, дабы удовлетворить все желания и предпочтения наших клиентов. Независимо от того, нужен ли вам мощный гаджет, новый телевизор либо умные часы, вы всегда найдете уникальное решение в нашей компании.

    ReplyDelete
  95. Если вы желаете заказать упоминания с конкретного закупить ссылки для продвижения сайта вебсайта впрямую, очень важно очередь выяснить его на наличие конкретных видов ссылок. Проще всего на данном ресурсе сыскать статью, избрать в ней бэклинк и взглянуть его в коде. Для сего кликните правой кнопкой мышки, откройте рационы, изберите «Посмотреть код»shameless В заключительных версиях CMS WordPress зачастую встречается тег nofollow noopener. Это также самое, именно и классический приспособление.

    ReplyDelete
  96. Специалисты фирмы владеют глубокими знаниями о продуктах Samsung http://www.ngo.ne.jp/userinfo.php?uid=31592 и также всегда рады поделиться с любым клиентом мощной информацией. Можно задать абсолютно любые имеющиеся вопросы, связанные с функциональностью, техническими параметрами и достоинствами какой угодно продукции.Практически во всех наши магазинах серьезный персонал, готовый оказать помощь и консультацию, в подборе и покупке необходимого вам устройства.

    ReplyDelete
  97. Ольга Лерман смотреть фото https://cojo.ru/devushki/olga-lerman-13-foto/

    ReplyDelete
  98. Брыков Василий 21 фото милые фото cojo.ru

    ReplyDelete
  99. Смешные картинки поздравления С Днем Рождения Марат картинки https://cojo.ru/kartinki/smeshnye-kartinki-pozdravleniya-s-dnem-rozhdeniya-marat-41-foto/

    ReplyDelete
  100. Прикольные авы подборка https://fotoslava.ru/prikolnye-avy

    ReplyDelete
  101. Райан рейнольдс короткая стрижка (47 фото) классные фото https://byry.ru/rayan-reynolds-korotkaya-strizhka/

    ReplyDelete
  102. Вид с террасы на воду (47 фото) HD фото https://fotoslava.ru/vid-s-terrasy-na-vodu-47-foto

    ReplyDelete
  103. Фиолетовые фотки (51 фото) красивые фото https://fotoslava.ru/fioletovye-fotki

    ReplyDelete
  104. Яна Сапета милые картинки https://fotoslava.ru/yana-sapeta

    ReplyDelete
  105. Lord God Wallpapers high resolution for free https://wallpapershigh.com/lord-god

    ReplyDelete
  106. Duke Basketball Wallpapers HIGH RES 100% free https://wallpapershigh.com/duke-basketball

    ReplyDelete
  107. R33 Skyline Wallpapers high resolution absolutely free https://wallpapershigh.com/r33-skyline

    ReplyDelete
  108. Zedge Christmas Wallpapers High Definition absolutely free https://wallpapershigh.com/zedge-christmas

    ReplyDelete
  109. Map Desktop Wallpapers HIGH RESOLUTION fast and free https://wallpapershigh.com/map-desktop

    ReplyDelete
  110. Gambar Keren 3D Minions Wallpapers high quality absolutely free https://wallpapershigh.com/gambar-keren-3d-minions

    ReplyDelete
  111. Привет, фанаты картинок и фото! Хочу порекомендовать вам галерею с 74 восхитительными фотографиями шоколадного лабрадора. Я сам только что просмотрел эту подборку, и она просто потрясающая! Каждая фотография передает неповторимый характер и очарование этих милых собак. Если вы, как и я, обожаете лабрадоров, то эта галерея точно для вас. Не упустите шанс окунуться в мир невероятной милоты и узнать больше о шоколадных лабрадорах. Лично я остался в полном восторге! Чтобы посмотреть все фотографии, перейдите по ссылке https://byry.ru/shokoladnyy-labrador/. Уверяю, вам точно понравится!

    ReplyDelete
  112. Приветствую! Хочу порекомендовать вам интернет-магазин fanwood.by, где вы можете найти фанеру ФК размером 2440х1220. Важно отметить, что в этом магазине вы найдете низкие цены на эту популярную продукцию. Я сам заказал фанеру в этом магазине, и она прекрасно подошла для моих строительных нужд. Рекомендую вам перейти по ссылке https://fanwood.by/shop/fk-fanera/ и приобрести фанеру ФК 2440х1220 уже сегодня.

    ReplyDelete
  113. Нацеди сиська лепка, ёпт! Эти мелкие братья-таксисты просто заебали всех своими невероятными талантами! Кажется, они своими лапками магию создания исскуства научились! Ты хоть знаешь, что такое такса арт? Нет?! Тогда скорей ко мне на страничку https://creofoto.ru/taksa-art, там тебя ждут прикольные фотки с участием этих малышей! Этот сайт просто охуенен, там ты увидишь, как таксы могут быть крутыми и стильными! Не веришь? Тогда проверь сам, дружище!

    ReplyDelete
  114. Привет, друзья! Хочу рассказать вам про классный сайт, где вы можете создавать крутые фото карандашом для срисовки онлайн! Там много разных фотографий, которые вы можете перевести в рисунки и потом сами их нарисовать. Это отличный способ развить свои художественные навыки! И самое крутое, что сайт совершенно бесплатный! Чтобы начать, переходите по ссылке https://risuemsami.ru/foto-karandashom-dlya-srisovki-onlayn/ и погружайтесь в мир творчества! Вспоминайте детство и начинайте рисовать уже сегодня! Удачи вам!

    ReplyDelete
  115. Я бы хотел порекомендовать интернет-магазин двп.бел. Здесь можно легко и удобно купить лдсп цена. Я недавно приобрел товары в этом магазине и был приятно удивлен качеством товаров и быстрой доставкой. Цены также оказались очень приемлемыми. Рекомендую всем, кто ищет надежного поставщика ДВП оптом или в розницу. Большой выбор и хорошее обслуживание гарантированы! Посетите https://xn--b1ad8a.xn--90ais/ и убедитесь сами!

    ReplyDelete
  116. Я очень доволен своей покупкой керамической плитки в интернет-магазине realgres.ru. Особенно хотелось бы отметить коллекцию Cevica plus, которая меня очень впечатлила. Красивый дизайн, высокое качество материалов и отличная цена - все это делает эту плитку превосходным выбором для моего дома. Благодаря реально широкому ассортименту я без труда смог найти то, что идеально подходит под мой интерьер. Быстрая доставка и отличный сервис - дополнительные плюсы данного магазина. Рекомендую всем обратить внимание на керамическую плитку Cevica plus и посетить сайт realgres.ru - https://www.realgres.ru/plitka-plus-cevica/.

    ReplyDelete
  117. Кроп с кудрями – это универсальная стрижка, которая актуальна не только на модных подиумах, но и в повседневной жизни. Этот стиль подходит для девушек с разной длиной волос и образует легкую и романтичную прическу. Кудрятся струи волосы, позволяющие создать безупречную текстуру и пышность. Кроп с кудрями сочетается с различными образами и стилями одежды. Если вы хотите попробовать эту стрижку или узнать о ней больше, рекомендую заглянуть на этот сайт https://cojo.ru/?p=592785, где вы найдете 45 фотографий кропа с кудрями для вдохновения.

    ReplyDelete
  118. Привет, друзья! Хочу поделиться великолепной коллекцией красивых картинок лебедей. Если вы любите наблюдать за элегантными и изящными птицами, то эта галерея точно для вас. Здесь вы найдете целых 85 фотографий, где лебеди прекрасно запечатлены в разных ракурсах и на разных фоновых пейзажах. Поверьте, картинки просто очаровывают своей красотой и изяществом. Не упускайте возможность окунуться в мир грации и прелести этих удивительных птиц. Чтобы насладиться просмотром, переходите по ссылке https://douo.ru/krasivye-kartinki-lebedi/. Уверен, вам понравится!

    ReplyDelete
  119. Привет! Рулетка, слоты, покер - это всё твои друзья в игровом зале? Тогда, бери на заметку этот сайт - https://cvam.ru/avtomat. Там есть огонь крутые автоматы, которые заставят твоё сердце биться быстрее! Зарегистрируйся, покажи свою удачу и тройной фастблат зафиксируют на тебе взоры у всех! Подними деньги и бегом на покерный турнир, только не забудь спросить меня, если нужны халявные советы ��. Чекай ссылку, не пожалеешь!

    ReplyDelete
  120. Это круто! Дайте вам немного советов по фотошопу. Если вы хотите добавить эффектный фон блики на свои фотографии, то обязательно загляните на этот сайт: https://cultmir.ru/fon-bliki-dlya-fotoshopa. Там есть огромный выбор разных фоновых бликов, которые подойдут для любого стиля и настроения. Просто скачайте нужный вам файл и добавьте его в Фотошоп. Нет ничего лучше, чем красивый фон блик, чтобы сделать вашу фотографию более интересной и запоминающейся. Проверьте это сами!

    ReplyDelete
  121. Привет, чуваки! Давайте поговорим о самом забавном и милом занятии - срисовке милых котиков! �� Если ты любишь рисовать и хочешь порадовать себя чем-то прикольным, то я нашел классный ресурс с крутыми картинками для срисовки, а еще и раскраски! Эти котики такие пушистые и милые, что прямо хочется их обнимать �� Не удержался и сам уже начал рисовать их. Кстати, вот ссылка на крутой сайт, где ты найдешь массу милых картинок для срисовки котиков и еще раскраски в подарок! Не упусти возможность окунуться в мир котомании �� https://risuemsami.ru/milye-kartinki-dlya-srisovki-kotiki-raskraski/ Посмотри сами, там куча вариантов и милоты на любой вкус! Удачной срисовки, братишки! ✌️

    ReplyDelete
  122. Приветствую всех! Хочу поделиться своим недавним опытом в интернет-казино Вавада. Я несколько раз слышал о нем от друзей, так что решил попробовать свою удачу. Зайдя на вавада рабочее зеркало vavadahch1, я сразу оценил удобный и интуитивно понятный интерфейс сайта. Зарегистрироваться оказалось просто и быстро, и в тот же день я получил свой приветственный бонус, а также несколько фриспинов. Захотелось сразу испытать удачу на слотах, и я не пожалел! Бонусы и крупные суммы не заставили себя ждать, а процесс игры вызвал только позитивные эмоции. Важно отметить, что выплаты проходят быстро и без проблем. Я действительно наслаждаюсь игрой на Вавада и хочу порекомендовать всем попробовать свою удачу! Если хотите начать играть прямо сейчас, перейдите по ссылке https://vavadah.site/.

    ReplyDelete
  123. Приветствую! Я хочу рассказать о своем недавнем выигрыше в интернет-казино Вавада. Меня зовут Алексей, и я долгое время искал надежное и честное казино для игры на деньги. Вот тут я наткнулся на сайт https://vavadaa.fun/, где нашел великолепный выбор слотов и щедрые бонусы. Вавада действительно порадовала меня простой регистрацией, быстрыми выплатами и удобным интерфейсом. К тому же, я получил отличный приветственный бонус и фриспины на свой первый депозит. И в итоге, благодаря удаче и крупным суммам, которые я выиграл, мне удалось повысить свое финансовое положение. Рад, что нашел Вавада, которая дарит столько радостных моментов и выгодных возможностей. Если тебе тоже интересна игра в казино, то я настоятельно рекомендую обратить внимание на Вавада. Бонусы на сегодня вавадаoffsite2 xyz тебя приятно удивят!

    ReplyDelete
  124. Йоу, народ! Вот у меня тут для вас парочка замечательных фоточек на поднятие настроения. Эти красивые картинки буквально працую волшебством! Если ты хочешь доброго дня и позитива, то как раз нашел, что нужно! Чтобы их посмотреть, кликай по ссылке https://cvam.ru/krasivye-dobrogo-pozitivnye и получай удовольствие! А потом не забудь поделиться своими эмоциями в комментариях. Держите себя в кайф, друзья!

    ReplyDelete
  125. Эй, ребята, всем привет! Если вы хотите сделать свой вечер еще лучше, то я знаю, как это сделать! Представьте себе: спокойная атмосфера, котята, милые и пушистые. Они такие милашки! А я знаю идеальное место, где можно найти море фоток с такими котятками. Просто перейдите по этой ссылке https://cvam.ru/kotyatami-4 и увидите все это красиво оформленное собрание котячих фоток. Не упустите шанс улыбнуться и расслабиться перед сном. Приятных снов! ����

    ReplyDelete
  126. жак мав каК

    ReplyDelete
  127. Привет, красавчик! Хочешь сделать так, чтобы молодожены до слёз растрогались от твоей открытки с поздравлением на свадьбу? Тогда тебе нужно скачать красивую открытку с поздравлением со свадьбой! Я нашёл для тебя отличный сайт, там есть самые стильные фото, которые подойдут для этого случая. Кстати, вот ссылка картинка с поздравлением со свадьбой стильные. Ну что, пошёл скачивать! Твои друзья будут в шоке от такого крутого поздравления!

    ReplyDelete

BLOG