Search This Blog

Wednesday, April 21, 2021

JAMANI ANKO - 5

  



Chombezo : Jamani Anko

Sehemu Ya Tano (5)


"likuneeeeeeee"

"lile jimama niliowaambie linalompenda joshua, sasa anataka kumuoa joshua"

Aliongea mama Kipenga

"weeeee acha utani"

"haaaaaa mie tena nina utani na nyie toka lini"

"enheee, ndoa lini hio"

"bado nime waacha wanaelewana ila lile jimama lile, linaonekana limedata kwa joshua... Mana yupo tayari kufanya lolote kwa mama joshua ili tu aolewe na joshua na azae nae watoto"

"jamani huyo mwanamke hana aibu jamani... Ana umri gani huyo mwanamke"

"weeeee, kizee kabisa, mimi mwanae"

"haaaaaaaaaa.. Jamani jamani, na mama joshua kukubali"

"ndio nimewaacha na mikasa yao"

"we nawe umeharakisha kuondoka"

"si nimewawahishia ubuyu ukiwa wamoto"

"nenda tena basi"

"badae, saizi ataniona mbeya"

Mama Kipenga sasa kajaaliwa kuwa mbeya, sasa hana wivu tena bali umbea sasa umemkaa kooni




Wakati huo tukija huku kwa akina Jessica, yaani nyumbani kwake jessica, mama yake alikuja tena leo....

"leo sijamkuta, hajaja"

Aliongea mama yake jessica, huku jessica akijibu

"ina maana mama umekuja ili umkute"

"ndio, nataka niwafumanie ili mfunge ndoa"

"heeeeee, sasa kama ni hilo mbona linawezekana, kuna haja gani mpaka utufumanie"

"leo nipeleke kwao nikakutane na familia yake.. Mana sitaki mtiane mimba afu muachane juu juu uteseke"

Aliongea mama Jessica huku Jessica akiwaza itakuwaje,...

"sawa, ila kuliko tumshtukize naomba nimpe taarifa ili aipange familia yake"

"sawa ila leo leo hii nataka iwezekane"

"mhhhhh mama, leo umeamka na nini leo"

"mimi sijui, mpigie... Mana pale nyumbani kwangu nina kitoto cha dada yako,.. Kacheza huko mimba chwiii... Haya aliomuoa sio aliompa mimba.. Na hataki mtoto.. Sasa nawewe wataka uniletee mtoto... Na ninavyo kuoa hapo una mimba wewe"

Jessica alishtuka kuskia hivyo, mana ni kweli ana mimba,..

"mama mimba nitoe wapi mimi"

"mimi ni mtu mzima, najua dalili za mwanamke mwenye mimba... Nyie dalili zenu mpaka mtapike ndio mjue mna mimba"

Jessica alishtuka, na hakutaka kubishana na mama yake mana huo ndio ukweli.. Alipiga simu kwa joshua, na wakati huo joshua yupo bafuni na simu ipo sebuleni.. Iliita ikakata, ikaita tena ikapokelewa...

"hallow joshua mpenzi"

"shkamoo"

"oohh marahaba ujambo"

"sijambo, kaka joshua anaoga"

"ooihh, sasa Mwambie mama, wifi anakuja na mama ake"

"haya, na kaka pia nimwambie"

"hapana usimwambie"

"haya"

Jessica alikata simu kisha akamsogelea mama yake na kumwambia,

"nime wapa taarifa"

"sawa"


Tukija huku ndani kwa mama joshua na mama sudi,... Sasa mama sudi amepewa nafasi ya kuongea anataka nini hasa


"mama joshua... Endapo utanikubalia, nitakununulia jumba la kifahari, nitakufungulia biashara unayotaka ya gharama yeyote na nitakununulia gari ya kutembelea,.. Hivi vyote nitavifanya ndani ya mwezi mmoja tu, naomba niolewe na joshua wako"


Aliongea mama sudi huku mama joshua akishtuka katika moyo wake, na kukumbuka maneno ya mtoto wake kuwa


"Mimi nimeshakua, sasa ni wakati wa kuachana na dhiki"


Hayo ni maneno ya joshua ambayo mama joshua aliyakumbuka...

"nisikilize kwa makini mama sudi... Kwanza kabisa, nimekubali vyote,.. Ila sitaki ufunge ndoa... Pili... Sitaki uzae na mwanangu,... Tatu.. Nataka mwanangu aoe binti lika lake,.. Na ujue kuwa ana mke.. Kingine, kama unataka kuishi nae.. Sawa ila sio kwenye ile nyumba yako.. Watoto wako wakija wamuone.. Jenga nyumba pembeni ambayo ni ya wewe na yeye... Ukikubali basi nami nakubali"


Aliongea mama joshua kisha akawa anaondoka,.. Mama sudi alimuita,

"basi njoo tuyamalize mbona madogo hayo.."

"ok Niambie umekubali lipi"

"sawa, nimekubali sitafunga nae ndoa, ila ataishi kwangu huko kwenye nyumba ambayo nitaishi nae.... Pili, huyo mke pia nataka ajue kuwa mimi nipo, ikiwezekana tupeane zamu za kulala, siku tatu kwake na siku tatu kwangu... Huyo mwanamke akikubali hio, basi hata mahari na gharama zote nitatoa mimi.... Kuhusu kuzaa, kwasababu atakua na mwanamke, basi naomba twende hospitali, nikaweke kitanzi mbele yako kabisa... Namimi nimekubali"

Aliongea mama sudi na mama joshua akafurahi, ila sasa ishu ni huyo mwanamke akubali kuwa na uke wenza..

"ok hapo kazi ni kwa huyo mwanamke kukubali uke wenza"

"hio kazi mpe mwanao aongee nae"

"sawa... Namimi ahadi yangu inatimilika lini"

"nimesema ndani ya mwezi huu kila kitu kipo tayari... Cha kufanya uniambie unataka kuishi wapi, unataka biashara gani, na utatumia gari aina gani... Na unipe majina yako matatu kwasababu ya kutengeneza hati miliki za nyumba na biashara na gari.. Alafu pia utakua karibu nami muda wote nikikwambia njoo utie saini zako"

"sawa... Ila joshua hutakutana nae mpaka unikabidhi mali zangu kwanza"

"jamani mama joshua, mbona unanifanyia hivi"

"ndio.. Nataka ufanye bidii yaani usije ukaleta kigeugeu"

"hapana, siwezi kugeuka"

"tuelewane, hutakutana na joshua mpaka unikabidhi,.."

"aaahhhhh ok, sawa, nitajitahidi, ila joshua nitamfuta shule kabisa ili awe namimi"

"mtajua wenyewe... Nenda ukaoge"

"sawa"

Mama sudi alifurahi sana kuskia hivyo...

Mama joshua kanogewa na mali sasa hataki kujua elimu ya mtoto wake....


Tukija huku kwa mama jessica, na Jessica wake,.. Jessica kwasababu anajua hali ya akina joshua, na anajua joshua ni mwanafunzi... Hivyo akatafuta njia ya kuahirisha safari, ili waende siku nyingine... Mama kwakua hajui, alikubali na mambo yakawa sawa, na hapo anavuta vuta joshua amalize kidato cha nne, ili waoane...


Wakati huo huku kwa joshua anatoka bafuni, anakutana na mama yake, anatabasam,.. Akajiangalia labda yuko uchi nini mana mama yake anatabasam huku akimuangalia,..

"mama vipi mmelewana vipi"

"kajiachia mwenyewe.. Mpe mkwaju ajiachie zaidi"

Joshua alishtuka mpaka akaachia ndoo na sabuni vikadondoka chini... Hakutegemea kama mama yake angeongea maneno hayo... Joshua hakutaka hata kumjibu mama yake, alienda mpaka chumbani kwake,.. Alishtukia kakumbatiwa na mama sudi kwa furaha akarushwa kitandani...

"mna nini nyie"

Aliongea joshua...

"mama joshua kakubali... Ila kasema tusioane, mana anataka uoe mke lika lako"

"kakubalije kubalije"

"atakawambia mwenyewe... Na nataka nitekeleze ndani ya mwezi huu mana kasema, sitaonana nawewe mpaka nimkamilishie hivyo vitu vyake"

"mmmmhhhh vitu gani hivyo"

"atakwambia... Njoo unitom****e tena, mana mwezi mzima huu sitakuona"

Joshua alimrukia tena mama sudi, safari hii aliichana chupi ile,.. Mchezo Ulianza upyaa...


BAADA YA MWEZI MMOJA KUPITA


Joshua akiwa zake shule, tena ulikua ni muda wa kutoka,.. Alimsubiri Jessica mpaka akafika...

"samahani mume wangu, nimechelewa"

"wala uaijali"

"Ulisema una maongezi namimi"

"ndio, si tunakwenda nyumbani"

"bwana mtoto wako anasumbua, chukua taxi, mi naona mbali"

"ushaanza kudeka, kimimba chenyewe kina mwezi na nusu basi unadeeeka"

"bwanaaa, basi nimekutania tu twende"

"uwe unafanya mazoezi"

"sawa mume wangu"


Walifika nyumbani, jessica alikwenda kuleta vinywaji kisha wakaanza maongezi.. Joshua alimwambia ukweli wote wa mama sudi,.. Mana jessica anajua mama sudi ni binamu yake.. Sasa kampa ukweli wote,...

"na alitaka nimuoe lakini mama kakataa,.. Sasa huyo mwanamke, akasema, basi amekubali nioe, lakini wewe ujue na yeye yumo, na mpangiane siku wewe na yeye"

Aliongea joshua lakini jessica alianza kulia huku akisema

"hivi leo umeamua kuniharibia siku yangu, na unataka nife na hiki kiumbe.. Mwanamke mtu mzima kama yule, mimi nishee nae mwanaume... Hapana.. Haiwezekani, nataka niwe nawewe tu, sitaki.. Kama ni shida nipo tayari kuishi maisha yeyote lakini niwe nawewe tu"

Aliongea jessica huku akilia sana,...

"jessica mke wangu.. Hata mimi sio kwamba nampenda,.. Na hapa nia yetu ni kupata pesa kisha tunahama mji... Sasa hivi sisi hatuishi tena pale.. Na sasa mama ana bonge la supamaketi... Na gari yake inakuja keshokutwa... Namimi kuna kampuni anataka kunipa iwe yangu,.. Sasa akisha nipa tu,.. Tumesha panga tunauza kila kitu kisha tunahama... Kwahio hilo ni jambo la muda tu,.. Na hata sasa yeye ndio anataka tuoane.. Ila niliogopa kukwambia ila leo ndio nakwambia, ni jambo la mpito tu"

"lakini mume wangu, huoni kwamba ni hatari sana"

"wala usijali, tulisha yajenga mimi na mama,.. Kikubwa ni wewe ukubali nikuoe keshokutwa tu.. Ila kazi yako ya ualimu utaacha,.. Namimi shule nitaacha"

"joshuaaaaaa... Nikiacha kazi itakuaje maisha yetu"

"Jessica... Kwa sasa tuna maisha mazuri.. Kwanza utatakiwa kwenda supamaketi na mama kule ukale mabumunda na mtoto wako huyu"

"mi naogopa huyo mwanamke ataniua"

"hawezi kufanya hivyo"

"lini tunafunga ndoa"

"wiki hii"

"nina furaha kuskia hivyo, ila kuwa uke wenza"

"Jessica mke wangu,... Yule ni kama hawala tu... Wewe ndio mke.. Na nimekwambia ni jambo la mpito nipewe hio kampuni nipite ivi"


Tukija huku nyumbani kwa mama sudi,.. Mama sudi alikua anacheka mno, afu yuko peke yake....

"hahahahahahahahahaha... Hahahahahah"

"hahahahahahahahahaahahahaha"

"uuuuuuwiiiiii hahahahahahah"

"hahahahaha asante mungu"

Wakati huo alikua anapata juisi baridi..

"hahahahahha mwanangu kunywa juisi"

Aliongea, lakini alionekana kama uchizi unamuanza... Mana hakukua na mtu hapo alipo...


Tukija huku kwa akina joshua.. Waaaaaoooo, wanaishi kwenye jumba la kifahari acha mchezo...

"hebu Niambie umesha ongea nae"

Mama joshua alimuuliza mtoto wake joahua baada ya kufika nyumbani

"ndio.. Amekubali lakini kishingo upande, hajapenda kabisa kwani hata hayo maisha yeye hana shida nayo"

"ungemwambia ni jambo la muda tu.. Mpigie simu sasa hivi Mwambie tuna jambo letu la muda tu"

"nimesha mwambia mbona"

"afya yake vipi lakini"

"salama tu,.."

"kajukuu kangu nataka kawe kakike"

Aliongea mama joshua akiwa na maana hata yeye anajua kuwa jessica ana mimba na sasa familia hizi tayari zimesha juana


Mara simu ya mama joshua inaita, kuangalia ni mama Kipenga

"heeee mama Kipenga habari yako"

"jamani mama joshua umehama hata hujaniaga jamani"

"usijali, tutatembeleana tu usijali"

"haya mwaya kisa umekua tajiri sasa hivi"

"bwana mama Kipenga acha maneno yako"

"haya mwaya... Mwanangu Kipenga harusi yake ni kesho..."

"wewe usiniambie mama kipe"

"ndio... Afu sitakwambia kumbe..."

"nini tena"

"kumbe huyo mchumba wake, ni mtoto wa tajiri huyo mmiliki wa mabasi..."

"heeeee,wacha weeee... Kwahio nawewe upo juu"

"aaah wapi, acha kunisanifu mama joshua"

"najua tutakutana sheli"

"hahahahahahaha, poa basi mimi nipo shamrashamra si unajua tena"

"haya mwaya... Joshua naye yake wiki hii hii"

"wewe acha utani mama joshua... Sasa na yule jimama au"

"hapana wewe, nani aoe mzee... Ana mchumba wake.. Na yule mwanamke kakubali"

Waliongea sana mama joshua na mama Kipenga majirani hawa, ila kwa sasa wamekuwa mbalimbali kulingana na maendeleo....


Tukija huku SEGEDA Dispensari alionekana mama sudi akiwa na furaha kubwa sana,... Mama segeda akamuuliza

"haya kulikoni mwenzangu"

Mama sudi hakujibu kwa mdomo bali alishika tumbo

"una maana gani mama sudi, unaharisha au"

"bora hata ningeharisha"

"una nini sasa"

"nina mimba"

"heeeeee... Mimba? Mimba imeingiaje na ulikuja na mama joshua nikaweka kitanzi"




"ni kweli... Ila hilo zoezi tulilifanya ikiwa tayari mimba imeingia... Siku tunapanga kuja huku, ndio siku nimegegedwa na joahua"

"yaani mama sudi unavyomuongelea huyo joshua, utafikiri unamuongelea mtu mzima mwenzio"

Aliongea mama segeda huku mama sudi akikasirika

"yaani mama segeda sijui ukoje, yaani hupendagi mambo yangu sijui kwanini... Mbona mimi sikufuatilii"

"sawa asante kwa kupata mimba... Si ndio unataka nikwambie hivyo.. Ila sio vizuri, mwache kijana wa watu aoe msichana lika lake"

"mbona keshokutwa anaoa na mahari nalipa mimi, nagharamia ndoa yao yote"

"hapo sasa nitakuunga mkono..."

"sawa ila huyu mtoto sitoi.. Mtoto wangu wa mwisho"


Tukija huku kwa mama joshua,... Simu yake iliita, kuangalia vizuri alikua ni mama sudi,..

"gari yangu itakua imeingia tayari"

Aliongea mama joshua kabla hajapokea simu... Kisha akapokea

"hallow mama sudi habari yako"

"salama mzima"

"mzima sjui wewe"

"safi tu,.. Vp joshua yupo hapo"

"anakula, mana katoka shule sasa hivi"

"aiiiiiiiiiiiiiiii"

"mama sudi una nini"

"mjukuu wako kanipiga teke"

Aliongea mama sudi kama vile ndio anamfikishia ujumbe....

"mjukuu wangu... Mjukuu wangu kivipi, mbona sijakuelewa"

"jamani mama joo... Nahisi nikuzae wewe au baba joo"

"mama sudi, hebu ngoja kwanza... Unataka kuniambia una mimba"

Aliongea mama joshua, afu mama sudi akamalizia hivi

"ya joshua"

"What??..... Mimba ya joshua,.. Umeipataje na uliweka kitanzi"

"tuliweka kitanzi ikiwa tayari mimba ipo ndani"

"mama sudi, Niambie ukweli, ulikutana na mwanangu tena"

"hapana, wala usimlaumu... Siku ile tulipofanyana pale kwako.. Nilokua kwenye siku zangu za hatari... Kwahio mimba iliingia siku ile ile"

"mungu wangu,... Kwanini tusiitoe mama sudi"

"weeeeee, mama Joshua... Naomba uniombe radhi, nampenda sana joshua,.. Na nitamzalia mtoto wake... Nyie fanyeni mipango yenu ya ndoa yenu,.. Na gari yako wiki hii itafika,.. Nataka niishi na mume wangu joshua tulee mtoto wetu"

Mama sudi Aliongea hayo, huku mama joshua asiamini masikio yake...

"lakini na huyo mke wake ana mimba nayeye"

Aliongea hivyo mama joshua ili kujaribu kumtikisa mama sudi, lakini walaaa hata hajali

"nilisha kubali uke wenza... Acha tumzalie joshua,.. Tena naona kama mnachelewa, mana toka siku ile sijaonana na mume wangu,.. Hebu afunge hio ndoa tuanze mkataba na mke mwenzangu"

Aliongea mama sudi kisha simu ikakata, mama joshua akabaki kuongea mwenyewe tu kuwa

"daahhhhhh, mwanangu ana kazi kweli"


Mama Joshua alimfuata joshua mpaka chumbani kwake

"aaaahhhh mama, kwanini unakuja bila hodi, sasa ndio nini hivi"

Aliongea joshua aliokua akibadili nguo,.. Sasa kakutwa akiwa na boxer tu....

"mshenzi wewe, nikuzae mwenyewe afu nikuogope..."

"lakini mama, nimeshakua mama... Unapaswa kuniheshim nikuheshim mama"

"uyo mwanamke mtu mzima unaemtafuna, humueshim ndio uniheshim mimi..."

"lakini wewe ni mama yangu, na unanua lengo letu kwake"

"hata kama... Na sasa nakwambia... Ana mimba sasa"

"nani ana mimba"

"mama sudi"

"heeeeeee..... Kumbe ni malaya"

"malaya?... Malaya wakati siku ile ndio ulimpa mimba"

"aitoe,.. Sasa mtoto ataniitaje na umri wake yule mwanamke"

"mtajuana wenyewe,.. Acha gari yangu ije.. Na umuoe jessica... Na ukishakabidhiwa hio kampuni,.. Tunauza kila kitu alafu maisha ni kenya"

"Kwahio tutakua wakenya"

"hebu vaa nguo uko.. Umbea tu.. Ndio mana umemrithi baba ako"

Aliongea mama joshua huku akiondoka

"hayo ndio madhara ya kuchungulia watoro zenu... Nimemrithi baba kitu gani sasa"

"we hujioni... Na watakuua nakwambia"

Aliongea mama joshua kisha akatoka zake nje....


"heeeeee, huyu mtoto kama baba ake... Kumbe ndio mana mama sudi anampenda kumanina zake huyu mwanamke"


Aliongea mama Joshua huku akicheka sana,..

"we wini, umefanya homework"

"ndio mama, tayari"

"sasa si ukalale, unaangalia makatuni tu hapa"

Alikua anaongea na mtoto wake wa kike aitwaye Winiflida, ambaye kwa sasa yupo darasa la tatu...

"sawa mama"


Wakati huo joshua naye ndio anatoka,

"haya nawewe wapi tena"

"si nakwenda kule ofisini, mana we mwenyewe upo huku, kule ni wafanyakazi tu, umewaamini sana"

"sawa we nenda... Nasubiri gari yangu niwe nakwenda na gari"

"mmmhhh haya mwaya"


SIKU ZILIKATIKA NA SASA NI MWEZI MMOJA BAADAE


"aaaahhhhhhhhh bwana Kipenga, Niambie ndugu yangu"

"salama tu hali vipi joshua"

"daahhhhh kitambo sana, mwanangu naskia tu Kipenga katoroka nyumbani mara hivi na vile.. Nikasema jamaa kapatwa na nini tena"

"aaahhh.. Maza alikua anazingua kinoma, ikabidi nijikatae Kwanza..."

"aiseee hawa wazazi nao wakianza kuzingua inakuwa tabu"

"enheee Niambie bwana joshua,.. Wiki mbili zilizopita nimwsikia umeoa, sasa nikawa sipo mjini hapa... Nilikua Nairobi kuna gari nilikwenda kuzisajiri kule sasa nikakosa nafasi"

Aliongea Kipenga, na kwa sasa kipenga alionekana wa tofauti sana....

"bwana ni kweli nimeoa wiki mbili zilizopita... Na sasa maisha sio mabaya"

"mmmhhh maisha sio mabaya wakati unatembelea VX mayai.."

"waapi ya mwanamke hio"

"yupi tena... Mana nawewe ndugu yangu kwa kuwakusanya"

"si yule jimama"

"jimama? Jimama gani tena... Sio yule binti kawa jimama tena"

"kumbe we hujui... Yule binti ni mwalimu wangu... Ila nina sponsa hilo balaa... Ndio linaniweka mjini"

"acha utani"

"aaahhhhhh, kama kawa"

"lakini najua hapo unacheza na akili, mana nakujua wewe akili zako hua hazipotei bure"

"kama ulijua vile bwana Kipenga.... Enhee nawewe vipi"

Waliongea mengi sana, waliulizana mengi mno, marafiki majirani, pia walisoma pamoja, ila Kipenga yeye alifeli, hivyo hakuiona sekondari... Ila joshua alifaulu


"mwanangu nilipomuacha maza.... Mara zali la kazi.. Mara mtoto huyu hapa.. Sikujua.. Kumbe ni mtoto wa bosa wangu,.. Afu nikajaa moyoni mwake.. Ndoa tulifunga mwezi uliopita... Mzew kanikabidhi majukumu yote, kwahio mimi ndio msimamizi wa hii kampuni, mimi ndio kila kitu"

"daaahhh hongera sana... Nadhani familia zetu kwa sasa zina furaha"

"acha kabisa joshua, nikikumbuka kipindi kile kijiweni, sina hata hamu"

"mwanangu Kipenga.... Tupambane tusirudi kuleeee"

"hicho ndio kitu ambacho kipo kichwani mwangu... "

"hata kwangu pia"

"mimi nakujua wewe akili zako haziendi bure"

"basi poa, kuna mishe nawahi mara moja tutakutana... Chukua namba zangu"

"poa poa nitakucheki bwana joo"

"aina noma"


Masaa yalisonga na sasa ni usiku wa saa mbili,.. Joshua akiwa nyumbani kwao na mke wake... Tena walikua wanakula... Ghafla simu ya joshua ikaita, kuangalia alikua ni mama sudi

"Hallo mpenzi, mbona huji.. Siku tatu tayari kwa huyo"

Aliongea mama sudi huku joshua akisema kuwa

"lakini si unajua mwenzio bado mgeni kwenye ndoa, acha nikae hata na kesho"

"weeeeeee, kesho mbali mume wangu.. Nataka uje leo, kwanza nina hamu"

Joshua akakata simu kisha akazima kabisa....


"ni nani huyo"

"ni yeye"

"ni hilo shuga mamy lako"

"sio shuga mamy.. Sema Sponsa"

"mmmhhh unavyobadilisha majina heeee"

"we kula ukalaze mimba hio"

"anasemaje"

"anasema eti nimepitiliza siku..."

"kwani yeye si hawala tu"

"achana nae"

Basi wakaendelea kula,... Dakika kumi mbali.. Mara honi ikalia nje ya geti...

"nani huyo saa hizi"

Jessica aliuliza, ila joshua keshajua ni nani mana honi ya hio gari anaijua

"jiandae kupigana, bondia kafika"

"bondia nani"

Joshua alitoka nje, kwenda kufungua geti, mana nyumba anayoishi joshua ndio nyumba hio hio anayo ishi mama yake... Ila zipo mbili ndani ya boma moja.. Hivyo hata geti wanatumia moja Kwahio mama sudi anapajua vizuri sana mana hio nyumba kanunua yeye japo hana umiliki nayo....

"nilijua tu utakuja"

"yupo"

"nani"

"mke mwenzangu"

"staki fujo"

"kiroo safi tu, anatakiwa ajue sheria za uke wenza"

"yupo ndani"

"baki nje nikamalizane nae"


Kabla hajamjibu mama sudi kaingia ndani, Jessica alishtuka kumuona mwanamke mjamzito kama yeye....

"wewe ni nani"

Jessica aliuliza mana hamjui kwa sura.. Japo kwenye harusi alikuwepo lakini hakujitambulisha yeye ni nani, ila mama sudi anamjua Jessica kupitia harusini...

"mke mwenzio"

"kumbe ni wewe, sasa umekuja kufata nini hapa"

"toka amekuoa ni siku ya ngapi sasa.. Wiki mbili, hajakwambia kuwa namimi nimo"

"kaniambia, lakini mbona wewe ni mkubwa hivyo"

Jessica alianza kumpondea mama sudi

"tuachane na mambo ya ukubwa.. Naondoka nae, hapa atarudi baada ya siku tatu.. Na zikiisha tatu kwako aje kwangu,... Kama hutaki tubanane hapa hapa kitanda hiki kimoja"

"sasa ngoja nikuulize... Kwanini usiishi na huyo aliokupa mimba"

"heheheheheheheehehe.... Mama weee, kilichopo hapo kwako, ndicho kilichopo hapa kwangu... Nipe jibu niondoke nae, au nikalete mabegi tuishi hapa"

Jessica anajua kweli, na aliambiwa akakubali... Mara sma ikaingia kwenye simu ya Jessica...

"USIHARIBU, FANYA UTAKALOWEZA ILA USIHARIBU, MPANGO WETU BADO HAUJAKAMILIKA,... VUMILIA NDANI YA MIEZI MIWILI TU.. UTAFURAHI MWENYEWE"


Message hio alitumiwa na joshua,...

"ok, sasa skia,.. Nakuahidi mimi mwenyewe, kesho namleta... Acha alale leo hapa.. Kesho nakuja nae nami nipajue kwako"

Aliongea Jessica, tena bila wasiwasi, alionekana naye kukubali kutafuta pesa mana kamuona mtu mwenyewe ni mzee sana hivyo, kivyovyote joshua hawezi kupenda mzee....

"una uhakika?? Nataka nikupe heshima yako ya ndoa... Na siku tatu zikiisha nami namleta mwenyewe"

"ok sawa.. Niachie kwa leo"

"sawa kwaheri usiku mwema"


Anatoka tu akakutana na joshua hapo nje

"tayari mmeongea..."

Aliuliza joshua japo kasikia kila kitu

"ndio... Kesho atakuleta... Na asipokuleta.. Nakuja na mabegi hapa... Hata mtoto wangu anahitaji malezi ya baba bwana"

Joshua alicheka mno

"we cheka tu"

Aliongea mama sudi huku akifungua geti mwenyewe....

"hahahahahahha... We toa gari achana na geti"

"Kwahio umefurahi mimi kuja kulia lia kwa mkeo...muone vile sura kama mtoto wake huku tumboni"

"sawa we nenda nitakuja kesho"

Basi mama sudi aliondoka na kutokomea zake....


"heeeeee, kumbe ni hili lizeee... Mimi nikajua kidogo atanitingisha, kumbe ni huyu"

Aliongea Jessica baada ya joshua kuingia ndani....

"we ulijua ni kabinti"

"ivi wewe umempendea nini yule mwanamke"

"kwani hujui"

"ivi mimi umenipendea nini"

"kwani hujui"

"ivi ukoje lakini mume wangu.. Kila kitu kwani hujui... Utajua mwenyewe na mzee wako... Wala hanitishi"


BAADA YA MIEZI SITA KUPITA


"mumeo bado hajarudi kazini"

Mama joshua alimuuliza Jessica,..

"bado hajarudi mama"

"mbona anachelewa sasa"

"lakini huu ndio muda wake"

Mama alikua ana jambo la kuzungumza na mtoto wake... Kwa sasa joshua anamiliki kampuni ambayo kapewa na mama sudi, yaani kaandikishwa kabisa yeye ndio mmiliki wake... Yaani anaamua yeye kwenye hio kampuni.. Ni moja kati ya kampuni anazomiliki mama sudi, hivyo katoa kampuni moja na kumpa joshua... Hizo zingine acha awabakizie watoto wake akina sudi na wengine... Joshua alimaliza kidato cha nne, lakini alijifelisha makusudi ili asiweze kuendelea na kidato cha tano kwasababu kama ni maisha tayari wanayo...

"piiiiiii"

"huyo nenda kafungue haraka"

Aliongea mama joshua lakini Jessica alikua kachoka sana, kwani mimba ilifikisha miezi 8 sasa...

"batuliii"

"abee mama"

"husikii honi huko"

"sawa mama"

Basi mfanyakazi alikwenda kufungua na joshua aliingia ndani,...


"Hebu kwanza kaa hapa"

"shkamoo mama"

"Marahaba, kaa sasa"

"shkamoo mume wangu"

"Marahaba vipi hali"

"salama tu...."

"sasa mama, kwanini nisioge kwanza"

"wewe mtoto.. Uoge umetoka kusukuma mikokoteni"

"daaaaahhhhh bimkubwa nae"

"eeeehhh eti bimkubwa nae... Kaa hapo"


Basi joshua alikaa sofani ili kumsikiliza mama anachotaka kusema....

"joshua?... Wewe ndio mlengwa haswaa... Tulichokua tunasubiri ni umilikishwe kampuni kisha tuondoke.. Lakini naona kimya mpaka sasa... Nimeshapata mteja wa supamaketi, na nataka nitafute mteja wa hii nyumba, na kile kiwanja chetu kule chini... Nawewe tafuta mteja wa hio kampuni, uza tuondokeni"


Aliongea mama Joshua, na kila mmoja alimsikia...

"ni kweli mama unacho ongea, na tulisha lipanga hili muda sana... Ila kupata mteja wa kampuni, sio jambo rahisi mama, hivyo kwanini usinipe muda kidogo"

"sawa, nakupa mwezi mmoja tafuta mteja uza... Nami wacha niuze kabisa ile supamaketi, tumkimbie huyu mtu"

"sawa mama"

Alijibu joshua kisha akawa anaamka... Lakini Jessica akawa na wazo...

"samahani mama, nina wazo kidogo kama hamtojali"

Joshua alirejea katika kiti ili kusikiliza wazo la Jessica....

"usijali mwanangu, unaweza kuongea tu"

Aliongea mama joshua

"Kwanini tunahama mjini, kwasababu gani"

Jessica aliuliza hivyo kisha mama joshua akamjibu

"ni kweli unapaswa pia kujua... Ila hii ni kwa usalama wako na wa joshua"

"kivipi mama, na nani atatudhuru"

"huyu mwanamke ambaye unapeana nae zamu za ndoa... Tunataka tuishi kwa uhuru"


"mama, samahani lakini... Mbona huyu mwanamke hana shida,.. Na nina uhakika hakuna wa kumdhuru hapa... Mimi mpaka sasa nina amani, wala hata hayupo akilini mwangu, kwanini tukaishi kwenye nchi za watu ingali mtu mwenyewe hana shida.. Mimi nimekubali kwa moyo mkunjufu, mume wangu akalale hizo siku tatu kwake,... Na nina amani kabisa, tena mwanamke mwenyewe hana shida, kukubwa tu nae apate haki yake japo hana ndoa... Kingine, yule mwanamke pale ana damu yenu, hata tukimkimbia bado ni bure,.. Mama? Kwanini tusiishi maisha yatu hapa hapa... Mana kama ni mali zote ni zakwenu na mna umiliki nazo, kuna haja gani ya kwenda kuishi kwa maficho wakati mtu wa watu keshajitolea ili tu alale na joshua siku tatu.. Mimi nimekubali,.. Samahanini lakini kama nimewaingilia"


Aliongea Jessica huku joshua akitikisa kichwa,...

"lakini ni kweli mama... Wazo zuri hilo pia mimi sioni haja ya kwenda kuishi kwa wasiwasi wakati mali ni zetu, hana uwezo nazo tena... Tunakimbia kwenda wapi"


Aliongea joshua huku mama akijibu kuwa

"nimewasikia vizuri sana wanangu... Mi nadhani sina budi kukubali, kwasababu lengo la kuhama ni ili niwape uhuru nyinyi, lakini kama mmeridhika na hii hali... Basi nami nasema hakuna haja ya kuondoka... Na hata kuuza sitauza tena"

Aliongea mama Joshua huku Jessica akifurahia wazo lake kukubaliwa...


"kwani mama una wasiwasi na nini haswa"

"kwa sasa sina wasiwasi kama mkwe wangu karidhika, basi, we kajifie mwenyewe huko"

Aliongea mama joshua huku joshua akijibu


"nani ajifie, mtu mwenyewe napiga moja hataki tena"

"we mshenzi unaongea ujinga gani mbele yangu"

"mmmhhhhhh basi mama yaishe,.. Nawe uko kama kigeugeu... Sasa si umeongea mwenyewe lakini"

"toa ushenzi wako uko.. Unapiga moja maana yake nini mshenzi, unaona mimi mkeo.... Huyu mumeo anavuta bangi siku hizi eeehh"

"sijui"

"atakua anavuta bangi mbwa huyu, anakosa heshima namimi anaongea upumbavu tu"

"msamehe mama hatarudia tena"

"mwambie ntamuachia laana huyu, mimi sio huyo mzee wake huko anaemparamia"

Mara joshua kurudi

"afu mama.. Nimesahau... Kile kiwanja chetu kule nataka nishushe bonge la hoteli"

"kazi kwako baba... Kiuno si unacho"

"umeona umeanza mwenyewe nikimalizia hapa utaanza kelele"

"naomba uende"

Joshua aliondoka huku Jessica akasema

"kumbe unamuanza mwenyewe ndio mana hehehe"

"nawewe lako moja na yeye"

"akuuuu"


Siku zilisonga maisha yakawa mazuri, hakukuwa na hofu tena,... Wala hakukua na mwenye hofu ya kuhama kwenda kuishi mbali....


Siku moja mama sudi alikuja kumtembelea mke mwenzie, Jessica

"heeeeee kwani siku tatu zimeisha"

Aliongea Jessica akidhani labda mama sudi kaja kumchukua joshua....

"achana na mambo ya siku tatu, kwanza hata wiki ukitaka kaa nae... Mimba yenyewe yanichosha tu afu bado niwaze mwanaume wanini"

"heheheheheheheehehe yamekua hayo.. Kwahio timbwili la siku tatu tena"

"nikimtaka nitakwambia aje... Sina hata hamu na mwanaume... Sijui ndio uzee unaingia"

"heheheheheheheehehe kwahio wewe hujioni"

"nitakuchapa wewe, mimi bado kijana..... Enhee Niambie, nimekuja kukusalimia nikajua tayari umesha jifungua"

Aliongea mama sudi huku akikaa kivivu kwenye sofa... Mana yeye na jessica wamepishana mwezi mmoja tu.. Jessica ana miezi 8 na masiku... Na mama sudi ana miezi saba na masiku...

"eeehh bado,.. Yaani naogopa, mama mkwe ananiambia bado wiki tatu tu"

"kazi unayo, ivi kumbe hujawahi kwenda leba eeeh?"

"iiiii mama weee, ndio ya kwanza hii"

"heheheheheheheehehe haloooooo.... Unalo ile bibi jessica"

"mbona wantisha ivyo"

"nakutisha au nakwambia, leba hakuna kutishana"

"hebu Niambie, kukoje kukoje... Ili nijipange.. Mana najua we mzoefu wa kule"

"tena sio mzoefu kidogo.. Mkongwe haswa, nina watoto watatu.. Huyu ni wa nne, napajua vizuri sana"

"enheee Niambie... Naskia ukishindwa kumtoa unapasuliwa"

"ndio"

"kwanini sasa"

"njia ndogo"

"afadhali..."

"afadhali kwanini"

"nina bonge la njia... Yaani nikifika tu pale.. Pyuuuu"

"heheheheheheheehehe ety pyuuuu, ehehehe, tutaona sisi na hio pyuu yako"

"sisi wenyewe na uzoefu wetu... Lakini tukikaribia tunawaza na kuwazua.. Wewe ndio ya kwanza ety pyuuuu... EHehehehehehe Jessica weee pole na pyuu yako"


"umekuja kwangu kunitisha au kunisalimia"

"we tuyaache hayo.. Mume wangu anarudi saa ngapi"

"saa 12 jioni"

"aje tu, nimemisi"

"kwahio unamsubiri"

"ndio"

"ndo ukapike, jiko lile"

"shika adabu yako mi mkubwa wako.. Naeshim tu hako kandoa kako"

"sasa si unanisaidia, mwenzio nimechoka ety"

"mtoto unajilegeza wewe... Ety ndio unasema ukifika leba Pyuuuu,... Eheheheheh"

"unaniuzi unavyocheka...."


"hodi humu.. Heeee mama sudi umekuja"

"ndio ma joshua habari yako"

"salama tu, naona wacheka kweli"

"mwali wako anichekesha kweli na pyuu zake, hebu Mwambie uyo"

"pyuuuu,... Pyuuuu ndio nini"

"enheheheheheheheheheh.. Muulize mwenyewe, mimi kuniacha hoi jamani mabinti hawa basi tu"


Ilikua ni furaha kubwa, na hata mama joshua kweli alijiridhisha kuwa mama sudi sasa hana nguvu, tena.. Kwani hio mimba ndio imemchosha kabisaaaaaa.... Maisha kwa sasa ni safi tu....


Tukija huku kwa akina Kipenga.... Kipenga alikua kamfumba mama yake macho, na kumfumbua....

"haya, unaona nini mbele yako"

Aliongea Kipenga huku mama kihisi haoni kitu...

"weeee, huku kwa mawaziri tumefuata nini kipenga"

"wewe ndio waziri sasa.... Mama hio nyumba ni yako kuanzia sasa"

Aliongea Kipenga, huku mama asiamini, machozi yalianza kumtoka....

"kidundo?"

"naama kaka"

"mama haamini... Shika funguo hizi hapa.. Nyumba yenu hio hapo... Mama hapo ndio kwako sasa,.. Na sasa nataka nikufungulie biashara, na gari lilee, ni lako.. Nitakutafutia mwalimu akufundishe gari"

Aliongea Kipenga lakini mama anakosa kitoa kauli mbele ya mwanae, amjibu nini.. Aongee nini, atoe shukurani gani.. Amuombe msamaha gani kwa yale matusi ya kipindi kile.... Mama Kipenga alibaki analia tu, mpaka kipenga anaondoka kwenda kupangilia kazi....

"kidundo??"

"naam kama"

"mpeleke mama ndani,. Mimi nitakuja jioni.... Kule msirudi tena.. Kwani humo kuna kila kitu,... Karibuni kwenye mji mpya"

Aliongea Kipenga kisha huyo akapanda gari yake na kuondoka... Mama Kipenga alihisi kuota

"mama, twende ndani"

"hivi kidundo, kipenga ananidanganya au"

"hapana mama.. Mimi mbona napajua kabla yako... Hapa ni kwetu na funguo hizi hapa"

Mama kipenga anashika funguo anafanya kutetemeka mikono, haamini kama na yeye ipo siku ataishi kwenye jumba la kifahari kama hilo..... Waliingia ndani lakini bado haamini


Tukija huku kwa akina jessica na mke mwenzie mzee...

"we pyuuuuu... Haya chakula kimeiva njoo ule"

"tueshimiane we mzee"

"mi mzee ningekuchukulia mume? Unalo ilo... We njoo ule"

Mama joshua alikua kwa pembeni anacheka tu...

"kula mwenyewe"

"utakosa nguvu za ku pyuuuu... Njoo ule hehehehe"


MWISHO....... MWISHO..... MWISHO......



0 comments:

Post a Comment

BLOG