Search This Blog

Sunday, April 18, 2021

HOUSEGIRL WA KITANGA - 1

  


IMEANDIKWA NA : KIZARO MWAKOBA

*********************************************************************************

Chombezo : Housegirl Wa Kitanga 

Sehemu Ya Kwanza (1)



Mimi ni msichana niliyekulia kwenye maadili ya dini ya kiislamu. Naweza kusema kuwa nawashukuru sana wazazi wangu kwa kunilea vizuri na kunifanya niwe mtoto mwema katika kijiji chetu cha Tanganyika kule mkoani Tanga wilaya ya Muheza. Wazazi wengi walikuwa wakitamani sana vijana wao wawe na tabia kama niliyokuwa nayo mimi.

MWANTUMU ndilo jina ambalo nilikuwa nimepewa na wazazi wangu siku ya saba baada ya kuzaliwa. Wakati mwingine nilikuwa nikiwasikia watu wakiniita TUMU. Hivyo nikakuzwa na majina hayo yaani Tumu ama Mwantumu.

Mzee Mohamedi ama wengi walizoea kumuita mzee Mudi pamoja na mke wake Bi.Zamda ndio walikuwa wazazi wangu walionileta hapa ulimwenguni pamoja na kunilea katika maadili mema.

Kawaida yangu huwa sipendi kujisifia hata kidogo, lakini kusema ukweli mimi nilikuwa ni msichana ambaye nilikuwa nimeumbwa na kuumbika vilivyo. Hapa sifa na utukufu tumpe muumba. Umbo langu lina urefu wa wastani yaani sio mrefu sana na wala sio mfupi wa kuchukiza. Uso wangu wa duara uliokuwa na rangi nyeupe mara nyingi ulikuwa ukipendezeshwa na mtindo wa nywele zangu niliokuwa nimezoea kusuka ambao wengi huuita twende kilioni. Macho yangu ya kusinzia niliyokuwa nikiyafumbua kwa taabu yalizidi kuvutia hasa pale nilipokuwa nikiachia tabasamu mara kwa mara na kuacha meno yangu madogo meupe yaliyokuwa na mwanya mdogo katikati kuonekana.

Umbo langu lilitaka kufanana na umbo la chupa ya bia. Juu nilikuwa mwembamba wa kawaida na kifuani nilikuwa na madafu mawili ambayo hayakuwa na ukubwa wa kuchukiza lakini pia hayakuwa madogo ya kujificha. Kuanzia kiunoni kushuka chini nilikuwa nimejazia vilivyo na kunifanya nivutie. Nyonga yangu ambayo ilikuwa ikitofautisha umbo langu la juu na la chini ilikuwa imetanuka mno kiasi cha kunifanya hata mimi mwenyewe kujitazama mara kwa mara hasa nilipokuwa pekeyangu chumbani.

Maadili niliyokuwa nimepata kutoka kwa wazazi wangu yaliniwezesha kuhitimu masomo yangu ya shule ya msingi katika shule ya msingi iliyokuwa ikifahamika kwa jina la Mkumbi nikiwa salama pasipo kuharibikiwa na tabia za makundi rika ambazo vijana wengi hukumbana nazo. Wasichana wengi wa kijijini kwetu hawakufanikiwa kumaliza shule kutokana na sababu mbali mbali kama vile kubeba mimba na wengine kufukuzwa shule kutokana na tabia zao ajabu ajabu.

Ingawa nilifanikiwa kuhitimu masomo yangu salama lakini naweza kusema sikuwa na bahati ya kuweza kuendelea na masomo ya shule ya sekondari. Siwezi kusema kuwa nilikuwa nimefeli mtihani, Laa hasha! bali kipindi kile shule za sekondari zilikuwa ni chache mno, hivyo wanafunzi wengi tuliishia elimu ya msingi na waliochaguliwa kuendelea walikuwa ni wachache.

****

Maisha ya kijijini hayakuwa na ujanja zaidi ya kilimo hasa kwa wale wenzangu na mimi ambao hatukupata bahati ya kuendelea na masomo. Zaidi ya kilimo kwa sisi wasichana tulikuwa tukisubiri siku ziende ili tuolewe basi.

Kusema ukweli mwenzenu mimi pamoja na kwamba nilikuwa nimekulia kijijini lakini jembe lilikuwa likinipiga teke kabisaaa. Nilikuwa nikienda tu shambani kwa lengo la kuwaridhisha wazazi wangu lakini nilikuwa nachukia sana kulima

Nakumbuka Jumapili moja nilikuwa njiani nikitokea shambani, nilikuwa nimepumzika chini ya mti mti mmoja mkubwa sana ambao kule Tanga tumezoea kuuita mvule ambao ulikuwa ukitoa kivuli kizuri. Nikiwa pale chini ya mvule alifika mwanamke mmoja ambaye nilikuwa nikimfahamu kwa jina moja tu la Mama Kibo. Mama yule ambaye naye alikuwa akitokea shambani alifika pale nilipokuwa nimeketi na kutupa jembe lake chini kwa kishindo.

“Ophhhh” Mama Kibo alipumua kwa nguvu, alikuwa na kila dalili ya kuchoka kutokana na kazi ya kulima pamoja na kutembea umbali mrefu.

“Pole sana mama” nilimpa pole mama yule huku nikitoa tabasamu la kumkaribisha kwenye kivuli kile cha kubembeleza usingizi.

“Ah! Ahsante mwanangu hujambo?”

“Sijambo mama Kibo, Shikamoo”

“Marahaba. Naona wapumzika mama” alisema mama yule kwa lafudhi ya kitanga.

“Jua kali mamaangu, ukishindana nalo hili laweza kukuua” nilizungumza ili kuonesha umuhimu wa mapumziko yale.

“Nikweli kabisa. Vipi leo mbona uko peke yako?” mama kibo alihoji huku akijiweka kwenye shina la mti ule wa mvule nakuegemea.

“Baba amekwenda Pongwe kuchukua maji, na mama amekwenda Muheza kuna vitu amekwenda kununua?” nilimjibu mama yule ambaye alionekana kutaka kufahamu walipo wazazi wangu ambao mara zote nilikuwa nikiongozana nao kwenda na kurudi shambani.

“Ahaa” mama Kibo alinijibu kisha akachukua kidumu cha maji kutoka kwenye kikapu chake na kukipeleka mdomoni. Nilimtazama mama yule jinsi alivyokuwa akiyabugia maji yale kwa pupa. Ilionekana alikuwa na kiu kwa muda mrefu ila alikuwa akitafuta pozi la kukituliza.

Alipomaliza kunywa maji yale alikiweka chini kidumu kile kisha akabehua kuashiria kuwa alikuwa ametosheka. Alipeleka mkono kinywani kujifuta majimaji amabayo yalikuwa yamemmwagikia mdomoni wakati anakunywa. Baada ya zoezi lile fupi aliinua macho na kunitazama usoni.

“Hivi mwanangu unampango gani?” alihoji mama Kibo kwa sauti ya chini.

“Mpango wa vipi mama Kibo?”

“Hapa kijijini”

“Mnh! bado sijakuelewa”

“Wategemea utaishi hivyo hadi lini?” alihoji mama Kibo kwa ile lafudhi yake ya kitanga.

“Kwani naishije jamani mama kibo, mbona kawaida tu?” nilihoji huku nikionekana nilikuwa bado sikuelewa swali lake.

“Kwanini wataka jizeesha na jembe mwana mdogo!”

“Mnh! mama Kibo bwana, jembe si ndo kila kitu hapa kijijini kwetu?”

“Si kweli!”

“Kumbe nifanyeje sasa?”

“Waonaje ukenda mjini?” Mama Kibo alihoji swali ambalo kwangu nililiona ni kama vile fumbo. Heti niende mjini! Sasa mimi binti niliyezaliwa kijijini Tanganyika na kukulia kijijini Tanganyika, huko mjini ningeenda kwa nani? na ningeenda kufanya nini?

“Sasa mjini nikafanye nini mama Kibo?” ilinibidi nimuulize vizuri mama yule ambaye nilimuona akizungumza maneno ya kusadikika na yaliyokuwa yamejaa pumba.

“Mwanangu mjini ndiko kwenye maisha” alizungumza mama Kibu huku akiokota kipande cha fimbo na kupigapiga chini kama vile anacheza.

“Mnh! mama Kibo bwana, kwani si hata hapa kuna maisha?”

“Kweli hata hapa kuna maisha, lakini mjini kuna maisha bora mwanangu. Kule hakuna kulima kama huku kijijini?” mama Kibo alizungumza maneno ambayo yaliniingia hasa pale alipogusia suala la kilimo. Nikameza funda la mate ya kutamani kuondoka pale kijijini.

“Sasa huko mjini mimi nitakwenda kwa nani?” nikahoji kwa hamasa.

“Wamfahamu yule dadaangu BI.FATUMA anayeishi Dar es salaam?”

“Ndio namfahamu”

“Si waona jinsi alivyo na maisha mazuri?”

“Ndio, nafahamu” nilijibu kwa upole huku nikisikiliza kwa makini maneno yake yaliyokuwa matamu kwenye masikio yangu. Kusema ukweli dada yake huyo aliyekuwa akimzungumzia alionekana kuwa na maisha mazuri. Alipokuwa akija pale kijijini kusalimia alikuwa anaonekana ni kijana kuliko hata mdogo wake mama Kibo kwa jinsi alivyokuwa anapendeza. Zawadi alizokuwa akiwaletea ndugu zake pale kijijini hazikuwa za kawaida. Kwa kigezo kile niliamini kwa asilimia tisini na tisa kuwa mjini kulikuwa na maisha mazuri. Na kwakuwa nilikuwa nachukia sana jembe basi ndio kabisaa nikazidi kuvutiwa na maisha ya mjini.

“Na mimi ningekuwa na ndugu Dar ningekwenda, maana kulima kushanichosha” Nilizungumza kwa sauti iliyokuwa imekata tamaa ya kuishi kijijini.

Mama Kibo alitoa tabasamu baada ya kuniona nimevutiwa na mazungumzo yake.

“Yule dadaangu ahitaji mfanyakazi wa ndani” alisema mama Kibo.

“Kwahiyo mie naweza enda huko Dar?” nilihoji kwa hamasa huku nikiinuka kidogo kuonesha kuvutiwa na taarifa ile. Nilikuwa tayari kwa njia yoyote ile ambayo ingewezekana ilimradi niondoke kijijini.

“Ndiomaana nimekwambia weye kwasababu najua waweza kaa na dadaangu kwasababu unatabia nzuri na heshima” mama yule alizidi kunitia hamasa kwa maneno yake yale ya kunipamba.

“Basi njoo nyumbani uzungumze na baba” nilimwambia huku nikonekana wazi kuwa nilikuwa na furaha juu ya taarifa zile.

“Usiwe na wasiwasi mwanangu jioni naja” mama yule alizungumza huku akijiinua na kusiamama. Namimi nilisimama na kujinyoosha viungo vyangu kisha nikachukua khanga niliyokuwa nimeitandika chini na kujifunga kiunoni tayari kwa safari ya kuelekea nyumbani. Tuliinua majembe yetu kisha taratiibu tukaanza kuondoka tukiwa na nguvu mpya iliyokuja baada ya mapumziko.

****

Taarifa za mimi kwenda mjini kufanya kazi za ndani zilipowafikia wazazi wangu, hawakuniwekea pingamizi chochote. Waliniruhusu niende mjini kwa dada yake mama Kibo kwasababu walikuwa wakifahamiana sana na mama yule. Nilifurahi sana ndani ya moyo wangu na kujiona nilikuwa nimeshinda kuepukana na adha ya mpini wa jembe pale kijijini Tanganyika.

Ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kufika jijini Dar es salaam tangu nilipokuwa nimezaliwa. Nilikuwa nimesimama kwenye bango moja la Cocacola ambalo nilikuwa nimeelekezwa nilipokuwa nikiondoka kijijini kwetu Tanganyika. Niliambiwa nisiondoke sehemu ile hadi mwenyeji wangu atokee kunipokea. Nami nikafanya kama ambavyo nilikuwa nimeagizwa.

“T u m u !” nilisikia sauti ya mtu ikiniita kutokea upande wa kushoto. Nilipogeuka nilimkuta dada yake mama Kibo akitembea kuelekea pale nilipokuwa nimesimama.

“Oooh mama!” nilihamaki kwa furaha. Sikupata taabu kumtambua kwasababu ni mara nyingi sana nilikuwa nikimuona alipokuwa anakuja kule kijijini kwetu Tanganyika kuwasalimia ndugu zake.

“Pole kwa safari mwanangu” alisema mama yule.

“Ahsante mama. Shikamoo”

“Marahaba, umesubiri sana enh?”

“Hapana mama nimeshuka sasahivi”

“Wahuni hawaja kusumbua?”

“Wamenisumbua lakini nilijitahidi kuwakwepa”

“Haya twende nyumbani mwanangu” alizungumza mama yule na kunisaidia begi langu dogo lililokuwa na nguo.

Tulipofika nje ya geti la Ubungo tuliingia kwenye Pajero moja kali sana ya rangi nyekundu ambayo ndiyo alikuwa amekuja nayo mama yule. Niliingia kwenye gari ile huku nikishangaa shangaa. “Ama kweli mjini raha” Nikajiambia ndani ya moyo wangu baada ya kuona msururu mrefu wa magari yaliyokuwa kwenye foleni pale kwenye mataa ya Ubungo. Majumba marefu na wingi wa watu vilinifanya nigundue utofauti uliokuwepo kati ya kijijini kwetu Tanganyika na pale jijini Dar es salaam.

Mama yule aliendesha gari lake kwa kunyata na kulibembeleza. Jamani nyie mjini kutamu, kijijini kwetu havikuwepo vitu kama vile. Kama nisingekwenda mjini mambo yale ningeyaonea wapi? Unadhani ningepanda lini gari kama lile la Bi.Fatma? Siwaongopei jamani mjini kuzuri, sio kama kwetu kijijini ambako nilikuwa nimezoea kuona ngedere na ndege. Mjini ni magari, mataa ya barabarani, na majumba marefu marefu hadi mbinguni. “Ooh Mama Kibo ubarikiwe sana, bila ya wewe nisingefika huku Ulaya” nilizungumza mwenyewe kimoyomoyo huku nikizunguusha macho kutazama majumba marefu.



Tulipofika nje ya geti la Ubungo tuliingia kwenye Pajero moja kali sana ya rangi nyekundu ambayo ndiyo alikuwa amekuja nayo mama yule. Niliingia kwenye gari ile huku nikishangaa shangaa. “Ama kweli mjini raha” Nikajiambia ndani ya moyo wangu baada ya kuona msururu mrefu wa magari yaliyokuwa kwenye foleni pale kwenye mataa ya Ubungo. Majumba marefu na wingi wa watu vilinifanya nigundue utofauti uliokuwepo kati ya kijijini kwetu Tanganyika na pale jijini Dar es salaam.

Mama yule aliendesha gari lake kwa kunyata na kulibembeleza. Jamani nyie mjini kutamu, kijijini kwetu havikuwepo vitu kama vile. Kama nisingekwenda mjini mambo yale ningeyaonea wapi? Unadhani ningepanda lini gari kama lile la Bi.Fatma? Siwaongopei jamani mjini kuzuri, sio kama kwetu kijijini ambako nilikuwa nimezoea kuona ngedere na ndege. Mjini ni magari, mataa ya barabarani, na majumba marefu marefu hadi mbinguni. “Ooh Mama Kibo ubarikiwe sana, bila ya wewe nisingefika huku Ulaya” nilizungumza mwenyewe kimoyomoyo huku nikizunguusha macho kutazama majumba marefu.

****

ENDELEA…..

Bi.Fatma alikuwa ni mwanamke wa makamo aliyekuwa ameolewa na mfanya biashara mmoja maarufu pale jijini Dar es salaam aliyekuwa akifahamika kwa jina la Sekiza. Mwanaume huyo alikuwa anamiliki maduka makubwa ya nguo na viatu yaliyokuwa mjini kariakoo na mengine Mwenge. Yeye Bi.Fatma alikuwa akiuza moja ya maduka hayo ambalo lilikuwepo Kariakoo.

Bi.Fatma na mume wake walibahatika kupata watoto wawili wa kiume amabao walikuwa ni Imran na Fadhili. Imran ambaye alikuwa ni wa kwanza kuzaliwa alikuwa akifanya kazi kwenye kampuni moja iliyokuwa ikijishughulisha na kudizaini matangazo na nembo za mashirika mbalimbali iliyokuwa ikifahamika kwa jina la KMC. Kampuni hiyo ilikuwa ikipatikana maeneo ya Posta mpya.

Fadhili ambaye alikuwa ni mdogo kwa Imran yeye alikuwa akiuza kwenye duka la viatu la baba yake lililokuwa maeneo ya Mwenge. Kijana huyu alipomaliza elimu yake ya chuo kikuu baba yake Mzee Sekiza akamkabidhi duka lile la viatu kusimamia. Kwa maana hiyo hakuwa na shida ya kuajiriwa mahali kokote kwasababu baba yake alikuwa akimlipa vizuri kuliko sehemu ambayo angekwenda kuajiriwa na watu ama mashirika mengine.

Familia hiyo ya Bi.Fatma na Sekiza ilikuwa ikiishi maeneo ya Mabibo karibu kabisa na sehemu ilipo hosteli ya Mabibo ambako wanaishi wanafunzi wanaosoma chuo kikuu cha Dar es salaam na DUCE. Pembeni ya nyumba yao walikuwa na fremu ambayo walimpangisha mwanamke mmoja wa kinyakyusa ambaye alifungua biashara ya kuuza chakula kwa wanafunzi waliokuwa wakiishikwenye hosteli hizo za Mabibo.

****

Utofauti uliokuwepo kati ya maisha ya kijijini na maisha ya mjini haukunisumbua sana awali kwasababu wakati wote nilikuwa ni mtu wa ndani ya geti. Sikuwa nimepata mwanya wa kutoka mbali na nyumbani. Mara nyingi nilipokuwa nikimaliza kufanya kazi zangu za mchana nilikaa sebleni kutazama runinga na nilipojihisi kuchoka niliingia chumbani kulala hadi jioni ambako niliamka na kuanza kufanya shughuli za jioni kama vile kuandaa chakula cha usiku.

Mara nyingi Fadhili yule aliyekuwa anauza duka la baba yake alikuwa akirejea nyumbani kula chakula cha mchana kisha anarejea tena dukani. Kwa kiasi fula nilijikuta nikifarijika na kuzoeana na kijana yule kuliko mtu mwingine yeyote pale ndani.

Umbo la Fadhiri lilikuwa ni dogodogo lililomfanya kuonekana kuwa na umri ambao ulikuwa unakaribiana kabisa na umri wakwangu mimi. Lakini hali halisi alikuwa amenizidi kama miaka mitano hivi.

Nilikuwa nikimpenda sana Fadhili kwasababu alikuwa ni kijana mstaarabu, mcheshi na mwenye heshima kwa kila mtu utafikiri alikuwa amekulia kijijini. Zaidi ya hivyo Fadhili alikuwa ni kijana mwenye muonekano mzuri ambaye alikuwa anapendeza sana akivaa nguo zake. Nisiongee sana jamani kusema kweli Fadhili alikuwa ameukosha mtima wangu. Najua utanishangaa ndugu msomaji kwasababu ilikuwa ni mapema mno, lakini sikuwa na kosa lolote kwani hata mimi ni binadamu na nina moyopia.

“Tumuuu!” Ilikuwa sauti ya Fadhili ikiniita nilipokuwa nimejipumzisha chumbani kwangu. Nilihisi moyo wangu ukipiga paaa! kutokana na hisia nilizokuwa nazo juu ya kijana yule ambaye sidhani kama alikuwa anafahamu lolote juu ya mawazo yangu.

“Abee” nikaitika kwa sauti ya kutoka usingizini huku nikijiinua kutoka pale kitandani. Nilichukua khanga na kujifunga kiunoni na nyingine nikajitanda kichwani kama ambavyo nilikuwa nimezoea kuvaa kule kijijini kwetu Tanga. Nguo zangu nyingi zilikuwa ni magauni marefu na khanga. Hivyo ndivyo nilivyokuwa nimefunzwa kuvaa kule Tanganyika kwetu.

Nilipotoka nikamkuta Fadhili amekaa kwenye kochi huku macho yake yakitazama kwenye mlango wa chumba nilichokuwa nimelala. Niliinamisha shingo chini kukwepa kukutanisha macho yangu na yake.

“Vipi dada ulikuwa umelala nini?” alihoji Fadhili

“Hapana kaka Fadhili sikuwa nimelala usingizi”

“Vipi umenisubiri sana enh?”

“Nimekusubiri hadi nikajiwa na usingizi”

“Dukani leo kulikuwa na wateja wengi sana, ndomaana nimechelewa” Fadhili alizungumza huku akiinuka kutoka kwenye kochi na kuelekea kulipokuwa na meza ya chakula.

“Sawa hamna shida” nilimjibu

“Vipi wewe umeshakula”

“Bado” nilijibu huku nikichezea vidole vya mikono yangu.

“Kwanini sasa ukae hadi saa hizi bila kula?” Fadhili alihoji huku nakinitazama na mkono wake wa kulia ukiwa umeshikilia kiti cha mezani pasipo kukivuta wala kukisukuma.

“Jamani kaka Fadhili mwenzio sijazoea kula pekeyangu” nilimjibu huku nikitoa tabasamu lililofanya ule mwanya wangu mdogo kuonekana.

“Haya njoo tule huko na mwanya wako” alinambia huku akivuta kiti.

Maneno yake yale yalinifanya kutoa kicheko kidogo ambacho kilimfanya naye kucheka pasipo na sababu ya msingi. Nilivuta kiti kilichokuwa mbele yake tukawa tumegeukiana yaani nikiinua macho namuona usoni. Alipakuwa chakula kwenye sahani yake kisha akanipa na mimi kijiko.

“Haya tuendelee” alinambia huku akifunua hotipoti iliyokuwa na mboga.

Nilichukua kile kijiko cha chakula na kujipimia kiasi ambacho kilikuwa kinanitosha. Fadhili akanisogezea hotipoti iliyokuwa na mboga. Nikasogea na kupakua mboga kwenye sahani yangu ya chakula.

“Haya Bismillah” Fadhili alisema na kuanza kula msosi ule niliokuwa nimeupika mimi.

“Mnh!” nikamsikia akiguna alipokuwa anameza chakula.

“Vipi kaka Fadhili?” nikahoji kwa wasiwasi nikiamini chakula hakikuwa kizuri.

“Mambo ya kitanga haya” alisema huku akitafuna chakula.

“Yepi tena kaka fadhili?”

“Madikodiko” alisema huku akimeza chakula alichokuwa anatafuna.

“Jamani kaka Fadhili wewe, mbona cha kawaida tu” nilizungumza huku nikinyonganyonga shingo yangu huku nikigonganisha gonganisha mapaja yangu pamoja. Midomo yangu niliing’ata na yale macho yangu malegevu nikayarembua.

“Vipi mbona hauli sasa?”

“Nala” nilijibu kwa lafudhi yangu ya kitanga.

“Wala enh?” Fadhili akanitania kwa ile lafudhi yangu.

“Halafu we Kaka Fadhili wanchokoza hivyo” nilizungumza huku nikitazama chini kwa aibu.

“Wala sikuchokozi mwaya enh! wenyewe twajilia madikodiko ya kitanga” Fadhili alizidi kuleta masihara huku nayeye akiwa ameinamisha shingo yake upande kama nilivyokuwa nikifanya mimi. Nikaangua kicheko ambacho kilikuwa kimejawa na aibu lukuki. Fadhili naye akacheka kwa kujilazimisha.

“Kula bwana mdogo wangu mi nakutania” Fadhili alizungumza huku akisogeza karibu sahani yake ya msosi na kukupiga vijiko viwili vya haraka.

Sikuwa nimefurahishwa na kauli yake ile ya kuniita mdogo wake. Nilihisi kama vile kulikuwa na kitu alichokuwa anataka kuninyima. Nilipenda sana aniite kwa jina langu.

Nikawa nimeinamia kwenye sahani yangu ya chakula huku nikimtupia jicho moja moja la wizi. kumbe na yeye alikuwa akifanya vile vile. Mara kadhaa tulikutanisha macho yetu na kutabasamu.

****

Kitendo cha kushinda nyumbani pekeyangu hakikuwa kinamfurahisha mama. Yaani Bi.Fatma. Asubuhi moja alipokuwa anataka kutoka kuelekea kazini aliniita.

“Hivi Tumu huwa unajisikiaje unaposhinda peke yako hapa nyumbani?” alihoji mama yule kwa sauti ya upendo.

“Kawaida tu mama huwa nikimaliza kazi nalala”

“He! kwahiyo unachokifahamu wewe ni kazi na kulala tu?”

‘Ndio mama mbona nimekwisha zoea” nilizungumza kwa kujiamini.

“Hapana usifanye hivyo. Kama ukiwa umemaliza kazi zako zote, unaweza kwenda hapo mgahawani kwa mama Bupe kujichangamsha, sio unajifungia ndani tu kama utumbo” alisema mama kwa msisitizo.

“Lakini mama mie nimekwisha zoea” nilijaribu kumueleza mama kwasababu huko alikokuwa ananiambia kwenda kukaa na kuzungumza nilikuwa sikuzoeana na mtu hata mmoja. Halafu ningezungumza nao kitu gani? wao ni watu wa mjini na mimi nilikuwa mtu wa kijijini. Hizo stori zingekwenda vipi. Kwa kigezo hicho sikuona sababu ya kwenda huko mgahawani kukaa na kupiga soga.

“Sasa mwanangu utakaeje ndani tu kama utumbo? toka nje angalau uoshe macho” mama alizungumza kwa upole.

Kwa kiasi fulani niliuona umuhimu wa maneno ya mama lakini kikwazo changu kikabakia pale pale. Nitakwenda kuanza vipi kuzungumza na hao wauza mgahawa waliopangisha flemu pale nyumbani. Hata hivyo nikaona hakukuwa na sababu ya kumbishia mama ingawa sikuwa nategemea kufanya vile alivyokuwa amenishauri.

“Sawa mama nimekuelewa” nilisema kwa upole.

“Haya mie natoka ila leo nitakuja na mgeni, usichelewe kuandaa chakula cha jioni” alizungumza Bi.Fatma kwa msisitizo.

“Sawa mama” nilijibu na kwenda kufungua geti.

Mama aliingia kwenye gari yake na kuiwasha, Alitoka kinyumenyume hadi nje ambako aligeuza na kuiweka barabarani tayari kwa kuondoka.

“Haya Mwanangu” mama aliniaga

“Sawa mama kazi njema” nilimjibu na kuanza kusukuma geti kulifunga huku mama naye akiondoa gari kutoweka katika mazingira ya nyumbani. Nilipomaliza kufunga geti niligeuka nyuma ili kuelekea ndani kuendelea na kazi. Nilimkuta kaka Imran amesimama hatua chache kutokea pale nilipokuwa nimesimama mimi. Kusema ukweli kaka Imran sikuwa nimemzoea kama ambavyo nilikuwa nimemzoea Fadhili. Nilikuwa nahofia hata kukutana naye kama tulivyokuwa tumekutana siku hiyo.

“Hee kumbe nawewe unatoka?” nilihoji haraka haraka ilimradi nimpite.

“Bado kidogo, nilikuwa nakutafuta wewe”

“Mimi?” nilihoji kwa wasiwasi.

“Ndio wewe”

“Sawa” nilijibu huku nikimsikiliza kwa makini nikiwa na hamu kubwa ya kutaka kufahamu kile alichokuwa ameniitia.

“Njoo ndani” kaka Imran aalizungumza na kugeuka kuingia ndani, nami nikamfuata nyuma huku nikiwa na wasiwasi tele ndani ya moyo wangu. Aliingia chumbani kwake na kuniambia nimsubiri sebleni. Baada ya dakika kadhaa alitoka akiwa ameshikilia mfuko wa Rambo mkononi.

“Chukua hii ni zawadi yako” alisema kaka Imran huku akinikabidhi kale kamfuko ka rambo.

“Yakwangu mimi?” nilihoji kwa kuhamaki.

“Ndiyo mdogo wangu nimekuletea wewe”

“Ahsante sana kaka Imrani” nilipokea mfuko ule huku nikihisi furaha ndani ya moyo wangu ingawa nilikuwa bado sikufahamu kilichokuwemo ndani yake.

“Usijali mdogo wangu” alisema kaka Imran na kutoka nje akiwa ameningi’niza funguo ya gari mkononi. Aliingia kwenye gari yake na kuiwasha kisha akapiga honi. Nilitoka na kwenda kumfungulia geti. Alitoa gari polepole na alipofika katikati ya geti akasimama na kuninyooshea mkono kuniaga. Huku nikiwa nimejawa na furaha kutokana na zawadi niliyokuwa nimeletewa namimi nilimnyooshea mkono kumuaga.

Nilifunga geti na kwenda ndani mbio. Nilichukua kale kamfuko nilikokuwa nimepewa na kuingia nako chumbani kwangu. Harakaharaka nilikafungua kwa hamasa kubwa. Nikakutana na nguo zimekunjwa pamoja. Furaha niliyokuwa nayo iliongezeka zaidi na kuanza kukunjua mojamoja ili kuzithaminisha. Kwanza kabisa mikono yangu ilikunjua nguo za ndani ambazo zilikuwa mbili. Nilifurahi sana nilipoziona nguo zile na sikuwa na hata chembe ya wasiwasi juu ya kitendo kama kile. Niliona ni jambo la kawaida sana na kuhisi kaka Imran alikuwa ameninunulia nguo za aina ile kama mdogo wake tu na si vinginevyo. Nilipofungua nyingine ndipo nikajikuta nikichoka mwenyewe. Nilikunjua kisketi kimoja kilichokuwa kifupi kuliko maelezo sijui ndio kinaitwa kimini? Ah sikuwa na uhakikika lakini kilikuwa ni kifupi mno.

“Mnh!” nikaguna mwenyewe huku nikikigeuza geuza mbele na nyuma.

“Sasa kaka Imran anionaje! mie ni wa kutembea uchi kweli?” nilijiuliza mwenyewe pasipo kujipatia majibu. Nikaiweka kiunoni sketi ile ili kuipima. Nilipobaini ilikuwa inaishia kwenye magoti nikasonya na kuitupa kitandani kisha kwa haraka nikakunjua ile ya mwisho iliyokuwa imebakia.

“Eboo!” nikashangaa kwa lafudhi ya kitanga baada ya kuikunjua na kuiona nguo yenyewe. Nguo ile ilikuwa ni blauzi ambayo ilikuwa na mikanda iliyopita kwenye mabega na kwa huku nyuma kulikuwa na uwazi wa kuonesha mgongo. Furaha yote ya kuletewa zawadi ikatumbukia nyongo. Nilihisi kama vile kaka Imran alikuwa amenidhalilisha kwa kuninunulia vinguo vya ajabu ajabu. Ile blauzi nayo nikaitupa kitandani kisha nikazisogelea zile nguo mbili za ndani na kuzishika tena. Niliachia tabasamu la matumaini kwasababu nguo nilizoziona zinaweza kunifaa ni zile tu. Lakini zile nyingine sikuzifagilia hata chembe.

“Hapa amepatia’ nilisema huku nikiikunjua nguo moja ya ndani kwa vidole vya mikono yangu kuithaminisha. Kwa mbele kulikuwa na viua vitatu vyekundu vilivyoendana sawia kabisa na ile rangi ya pinki ya nguo yenyewe.

“Hodiii” nilisikia sauti ya mtu kutokea nje ikibisha hodi.

“Karibuu” niliitika na kutoka nje haraka.

Nilifungua geti dogo na kumkuta BUPE yule mama wa kinyakyusa aliyekuwa akifanya biashara ya mgahawa kwenye fremu ya pale nyumbani.

“Karibu” nilimkaribisha mara tu nilipofungua geti.

“Aksante, hujambo wewe?”

“Sijambo shikamoo”

“Naomba uniazime chaja ya nokia” alisema mama yule.

Sikutegemea kama shida yake ingekuwa ni kuazima chaja ya simu. Nilitulia kidogo kama vile nikitafakari jibu la kumpa.

“Usiwe na wasiwasi binti, huwa ninaazima” alijieleza mama yule. Nilimtazama kwa sekunde kadhaa huku nikitafakari nitoe ama nisitoe. Sikuwa nimepewa ruhusa ya kuazimisha vitu vya mule ndani. hata hivyo nikakumbuka mama alipoondoka alinitaka niende kukaa kwa mama yule, hivyo nikaona isingekuwa vibaya kumpatia.

“Ngoja niangalie kama ipo” nilisema huku nikiingia ndani.

“Ipo bwana, kila siku nakuja kuazima” alisema Bupe kwa kujiamini.

Kwa bahati nzuri nilifanikiwa kuiona chaja ile pale sebleni. Niliichomoa na kuja kumkabidhi.

“Ahsante binti”

“Haina shida”

“Kumbe unaitwa nani vile?” alihoji mama yule huku akinichekea chekea

“Mwantumu au Tumu” nilijibu.

“Unatokea wapi?”

“Tanganyika” nilijibu kwa kifupi.

Jibu langu lilionekana kumchanganya mama Yule. Akatulia kwa sekunde kadhaa huku machp yake akiwa ameyakazia aldhini. Alipoinuka akahoji tena.

“Tanganyika ndio wapi?”

“Kijiji chetu kinaitwa Tanganyika”

“Ni mkoa gani?” Mama Yule wa kinyakyusa alizidi kuhoji maswali ambayo nikahisi yakianza kunikera.

“Tanga” Nikajibu kwa ufupi.

“Mnh! kwahiyo wewe ni binti wa kitanga?” alihoji mama yule huku akitabasamu.

Sikumjibu kitu zaidi ya kucheka tu huku nikiwa nimeinamia chini kwa aibu.

“Watokea Tanga mapenzi yaliko zaliwa, inabidi uje unipe somo na mimi niwe fundi” Bupe alizungumza na kuondoka huku akicheka cheka kama mwehu. Wala hakuwa amenifurahisha na vile vineno vyake vya ajabu ajabu. Heti natokea Tanga mapenzi yaliko zaliwa. Mara Ooh nije namimi unipe somo niwe fundi, Kwani mimi ndio somo wa mapenzi? Mtu mzima Hovyoo!” Nilizungumza pekeyangu huku nikifunga geti.



“Kumbe unaitwa nani vile?” alihoji mama yule huku akinichekea chekea

“Mwantumu au Tumu” nilijibu.

“Unatokea wapi?”

“Tanganyika” nilijibu kwa kifupi.

Jibu langu lilionekana kumchanganya mama Yule. Akatulia kwa sekunde kadhaa huku machp yake akiwa ameyakazia aldhini. Alipoinuka akahoji tena.

“Tanganyika ndio wapi?”

“Kijiji chetu kinaitwa Tanganyika”

“Ni mkoa gani?” Mama Yule wa kinyakyusa alizidi kuhoji maswali ambayo nikahisi yakianza kunikera.

“Tanga” Nikajibu kwa ufupi.

“Mnh! kwahiyo wewe ni binti wa kitanga?” alihoji mama yule huku akitabasamu.

Sikumjibu kitu zaidi ya kucheka tu huku nikiwa nimeinamia chini kwa aibu.

“Watokea Tanga mapenzi yaliko zaliwa, inabidi uje unipe somo na mimi niwe fundi” Bupe alizungumza na kuondoka huku akicheka cheka kama mwehu. Wala hakuwa amenifurahisha na vile vineno vyake vya ajabu ajabu. Heti natokea Tanga mapenzi yaliko zaliwa. Mara Ooh nije namimi unipe somo niwe fundi, Kwani mimi ndio somo wa mapenzi? Mtu mzima Hovyoo!” Nilizungumza pekeyangu huku nikifunga geti.

ENDELEA


****

Kama ambavyo nilikuwa nimeagizwa na Bi.Fatma. Nilikuwa nimeandaa chakula cha jioni mapema sana. Jioni ile mama alikuwa amekuja na msichana mmoja ambaye alikuwa ni mtoto wa dada wa mume wake Sekiza. Jina la msichana yule lilikuwa ni Mainaya.

Mwenyewe alikuwa anafanya kazi kwenye shirika la simu la VODACOM. Mara kwa mara alikuwa anakuja pale nyumbani kwa mjomba wake kusalimia.

Ingawa Mainaya alikuwa bado hajaolewa lakini umri wake ulikuwa ni mkubwa kuliko umri wa Fadhili. Mainaya alikuwa amepishana kidogo sana na kaka Imran. Hivyo umri wake ulikuwa upo kati ya umri wa Fadhili na wa kaka Imran.

Mainaya alikuwa ni muongeaji kuliko hata alivyokuwa Fadhili. Naweza nikasema alikuwa ni mcheshi kupitiliza. Ndugu zake walikuwa wanampenda sana binamu yao huyo. Mara nyingi walipokuwa pamoja hawakuogopana kuzungumzia jambo lolote.

Baada ya kumaliza kula chakula cha jioni, mama na baba walikwenda chumbani kwao kupumzika. Pale sittingroom tulibakia mimi, Fadhili, kaka Imran, pamoja na dada Mainaya. Tulikuwa tukitazama tamthiliya kwenye runinga huku Mainaya na Fadhili wakituchekesha kila mara. Uwepo wa Mainaya ulipoungana na uwepo wa Fadhili pale ndani, hakika nyumba ilichangamka.

Mara kwa nara macho yangu yaligongana na macho ya kaka Imrani ambaye niligundua tofauti kwenye sura yake. Alikuwa akinitazama kama vile kulikuwa na kitu anataka kuniuliza lakini aliwahofia ndugu zake. Nikajitahidi sana kukwepesha macho yangu kukutana na yakwake. Kwanza nilikuwa nikimuogopa sana hata sikujua ni kwanini. Halafu vile vinguo vyake vya ajabu ajabu alivyokuwa ameniletea havikunipendeza moyoni hata kidogo.

Uchovu ulinifanya nianze kusinzia pale kwenye kochi nilipokuwa nimekaa. kwakuwa tamthiliya iliyokuwa ikiendelea ilikuwa imeninogea, nilijivuta na kujilaza kwenye kochi huku nikitazama runinga. Usingizi mwanaharamu jamani, ulinichukua pasipo kujitambua palepale kwenye kochi.

“Vipi Mwantumu amelala nini?” nilishituka usingizini baada ya kusikia jina langu likitajwa na Mainaya, hata hivyo sikufumbua macho nikajifanya bado nimelala.

“Sasa si akalale ndani” alisema Fadhili kwa sauti yake ya ucheshi ambayo iliniburudisha sana.

“Ah! mwacheni bwana apumzike, usingizi wa sebleni unanoga kuliko wa chumbani” nikamsikia kaka Imrani akitoa hoja yake.

“Shangazi naye ameanzaje kuleta mrembo kwenye nyumba yenye midume mitupu, tena haijaoa” alisema Mainaya kwa masihara.

“Mrembo wapi! kitoto tu hicho” alisema Fadhili kwa dharau.

Safari hii maneno ya Fadhili hayakuwa yameninogea, heti mimi nilikuwa katoto. Alinikera sana ndugu msomaji nisikufiche.

“Kitoto! wewe si ndiye unayesema. Pengine hapo alipo hana kitu” alisema Mainaya maneno ambayo sikuyaelewa. Hata hivyo sikufumbua macho, nikajifanya kujigeuza na kupumua kwanguvu utafikiri nilikuwa kwenye usingizi mzito.

“Hilo ni umbo tu Sister, hicho bado kinanuka mkojo” Fadhili alizidi kutetea hoja yake kwa kuzungumza maneno ya shombo. Hapo sasa ndipo nikabaini sababu ya Fadhili kuto kunitongoza ingawa nilikuwa nikijitahidi kumuonesha kuwa nampenda.

“Sikia mdogo wangu, sikuhizi hakuna watoto. Tena kwa binti mrembo kama huyu sidhani kama huko kijijini kwao watakuwa wamemuacha salama” Mainaya naye alizidi kunikomaza mtoto wa mwanamke mwenzie.

“Aisee mimi sikubaliani na wewe hata kidogo. Kitoto cha watu kinaonekana hakijui hata kufua nguo yake ya ndani” Fadhili alizungumza maneno mabaya nyie. Sasa si dharau hizi? heti nilikuwa sijui hata kufua kufuli langu. Mnh! haya bwana. Mtoto wa kike nikaendelea kula jiwe pale kwenye kochi.

“Heti kaka Imrani mwenzetu we unasemaje?” Mainaya alimhusisha kaka Imrani ambaye muda wote alikuwa kimya akiwasikiliza.

“Japo ni kadogo lakini kanalika” kaka Imrani alitoa jibu ambalo sikulitegemea.

“Utakalaje haka jamani kananuka shombo?” alisema Fadhili.

“Unakatia ndimu na pilipili kibao, shombo lote linakata” alisema kaka Imrani na kuwafanya Mainaya na Fadhili kuangua kicheko. Nilikuwa namuona kaka Imran sio muongeaji kumbe akiwa kwenye anga zake alikuwa ni hatari! Ingawa alikuwa akitoa moja moja lakini yalikuwa ni madongo ya uhakika.

“Umeona kaka Imran. Yaani huyu mtoto akipata viwalo vya kimjinimjini na matunzo mazuri. Wenywe humu ndani mtakimbizana” alisema Mainaya na kuwafanya Fadhili na kaka Imrani kuangua vicheko. Hata sijui walikuwa wanacheka nini maana mimi nilikuwa sielewi utumbo wao waliokuwa wanauzungumza.

“Mimi nawaambia hata kama kaweje sikatongozi, haka” Kaka Fadhili alimalizia kicheko chake kwa maneno yake ambayo mimi niliyaona yamejaa kejeli na dharau. Ndugu msomaji usiombe kupokea maneno ya kejeli, dharau na kashfa kutoka kwa mtu ambaye unampenda. Niliumia sana usiku ule.

“Jamani hebu muamsheni akalale ndani mrembo wa watu” alisema Mainaya huku akimalizia kucheka.

Fadhili aliniita kama mara mbili hivi, ndipo nikaamka na kujifanya nimetoka kwenye usingizi mzito sana ambao bado ulikuwa umenikamata. kumbe utumbo wao wote nilikuwa nimeunyaka.

****

Maneno ya Mainaya na kaka zake yalinifanya nikose usingizi usiku wa siku ile. Nilitumia muda mwingi kuutafuta usingizi pasipo na mafanikio. Niligalagala huku nikiwa nimefumba macho kulazimisha nilale lakini sikuweza kabisa.

Nikiwa najipindua pindua kitandani pale nikasikia mlango wa chumbani kwangu ukigongwa kwa sauti ndogo. Mwanzo niliogopa kidogo lakini baada ya muda niliinuka na kwenda kuwasha taa. Nikasogea malangoni na kushika kitasa cha mlango kisha nikaweka sikio langu la kulia kwenye tundu ya kitasa kile.

“We nani?” Nikahoji kwa sauti ya chini ambayo bado ilikuwa na woga.

“Ni mimi fungua” nilisikia sauti ikijibu kwa kunong’ona lakini sikuweza kuitambua ilikuwa ni sauti ya nani. Nilichukua khanga yangu iliyokuwa ikining’inia kwenye msumari na kujifunga kwenye kifua kisha nikausogelea tena mlango.

“We nani?” nikahoji tena

“We fungua tu utaniona” alisema mtu yule kwa ile sauti yake ya kunong’ona.

Pamoja na kwamba nilikuwa bado sikumtambua mgeni yule lakini nikafungua mlango kwa tahadhari kubwa sana huku moyoni nikiwa na wasiwasi.

Nilipofungua tu mtu yule aliingia chumbani kwangu moja kwamoja. Nilipomtazama vizuri nikamtambua. Kumbe alikuwa ni kaka Imran. Alikwenda mojakwamoja na kuketi kitandani.

“Funga mlango” akaniambia kwa ile sauti yake ya kunongo’na.

Niliurudisha mlango ule pasipo kufunga kwa komeo. Ndani ya moyo wangu kulikuwa kumejawa na wasiwasi kibao. Kitendo kile hakikuwa cha kawaida kwa mtu ambaye nilikuwa namheshimu kuliko kawaida kuingia chumbani kwangu usiku mkubwa kiasi kile halafu heti ananiambia nifunge mlango. Jamni nyie acheni tu, Duniani kuna mambo!.

Baada ya kurudisha malngo niligeuka na kuegemea kwenye mlango ule huku macho yangu yakitazama chini kwa aibu. Kaka Imrani alinikazia macho kisha akameza funda la mate.

“Vipi mbona kama unaogopa?” alihoji

“Hapana” nikajibu kwa wasiwasi.

“Haya njoo basi tuzungumze”

“Zungumza tu nakusikia” nikamjibu kwa sauti ya chini huku macho yangu yakiwa angali yanatazama sakafuni. Kaka Imrani akanitazama na kutoa tabasamu.

“Inaonekana ni muoga enh?”

“Hamna” nikajibu nilijibu huku nikibonyeza bonyeza vidole vya mikono yangu.

Kaka Imrani aliinuka kutoka pale kitandani kwangu na kunisogelea mlangoni ambako nilikuwa nimesimama.

“Ondoa wasiwasi jamani mimi nilikuwa nataka tu kufahamu kama ule mzigo niliokuletea ulikupendeza” Kaka Imran alizungumza kwa sauti ya chini wakati akinisogelea.

“Asante nimezipenda” Nikamjibu huku nikimpisha pale mlangoni na kusimama pembeni.

“Sasa kama ulizipenda mbona hukuniambia hadi nikuulize?” alisema Imran akiwa amesimama hatu achache kutokea nilipokuwa nimesimama mimi.

“Ningekwambia tu kaka” nikajibu kwa aibu.

“Unaweza kuzivaa nikuone kidogo?”

“Abee!” nikaitika kama vile nilikuwa sikusikia maneno yake yale ya kushangaza.

“Namimi nataka kuona jinsi zilivyokupendeza mtoto mzuri”

“Mnh” nikaguna kwa kwa wasiwasi.

Yaani vile vinguo vyake vya ajabu ajabu alivyokuwa ameniletea ndivyo alikuwa anataka nivivae mbele yake. Kwakweli ulikuwa ni mtihani mgumu sana mbele yangu. Tena kwa vile ambavyo nilikuwa namheshimu kaka yule, Hata kama ni wewe ndugu msomaji naamini usingeweza. Mtoto wa watu nilikuwa nimekwishazoea kuvaa magauni na sketi ndefu, halafu yeye ananilazimisha kuvaa vinusu uchi, Eboo! Hana haya!.

“Vipi mbona unaguna” kaka Imran akahoji.

“Nitavaa kesho” nikaongopa.

“Kesho mie naondoka asubuhi sana, kwanini usivae sasahivi?”

“Mnh!”

“Sasa unaguna nini?”

“Lakini mbona nilikwisha jaribisha mchana”

“Ndio sikatai, lakini mimi sijakuona ulipojaribisha”

“Sawa kaka lakini….” Nilisita kuzungumza

“Lakini nini?”

“Nguo zenyewe mbona ndogondogo vile” nikazungumza la moyoni.

“Ndogo?” Kaka Imran akahoji kwa mshangao.

Nikajibu kwa kichwa pasipo kuinua mdomo wangu.

“Ndio, kale kamoja kanaishia humu kwenye mapaja, na kale kengine huku mgongoni kote kapo wazi” nikazungumza ukweli motto wa kike.

“He!” kaka Imran akabaki mdomo wazi kwa mshangao

“Haki yamungu vile”

“Sasa nawewe mrembo, zile ndio katalogi za mjini. Inamaana we huoni kwenye TV wanavyo vaa?” Kaka Imran akazungumza kwa sauti ya chini.

“Akuu! Mie siwezi” nilizungumza huku nikipandisha bega moja juu kuonesha msisitizo wa kupinga kile alichokuwa anakitaka.

“Hebu vaa basi kidogo tuone”

“Hapana kaka Imran mie siwezi”

“Unajua zile nguo zimenunuliwa kwa bei mbaya?”

“Sijui, labda niwe navaa na khanga juu” Nikamwambia.

“Khanga za nini wewe? hapa mjini” Alizungumza kaka Imran huku akiangaza angaza macho yake chumbani mle kama vile alikuwa anazitafuta zile nguo nilipokuwa nimeziweka.

“Ziko wapi hizo nguo zenyewe?” alihoji

‘Kule kwenye kabati”

“Hebu zilete" alinambia.

Nikiwa bado na woga nikavuta hatua kuelekea kwenye kabati kumtolea vile vinguo ambazo mwenyewe alikuwa akiviita nguo. Nilipopita karibu yake akanidaka mkono na kunisimamisha.

“Hebu ngoja kwanza mtoto mzuri” alizungumza huku akinivuta mkono wangu. Nilisogea na kusimama karibu kabisa na pale alipokuwa amesimama yeye.

“Mbona unataka kuniangusha jamani mrembo” alinambia

“Kwanini”

“Inamaana wewe hutaki kupendeza?”

“Abee!”

“Hupendi kupendeza?”

“Napenda”

“Sasa kwanini unapenda kujivalisha kizee?”

“Abee”

“Haya nambie na zile Chuchurichu nazo pia hujazipenda?”

“Mnh chuchurichu ndio nini?”

“Aah zile za ndani bwana!” alihoji kaka Imran swali amablo kwakweli sikuwa nimelitegemea hata kidogo. Nikabaki kimya nikitoa tabasanu pasipo kuzungumza neno lolote.

“Heti mtoto mzuri, nijibu basi” Kaka Imrani alizungumza huku mkono wake wa kushoto akiwa ameupeleka kwenye kichogo changu na kupapasa nywele za shingoni.

“Nimezipenda” nilijibu huku nikibonyea chini kwa mshituko kutokana na kitendo cha kaka Imran kunitekenya nyuma ya shingo.

“Unaweza kuzijaribu namimi nione zilivyokupendeza?” kaka Imrani alizungumza kwa sauti ya chini zaidi ambayo ilikuwa kama vile ikinibembeleza.

Mnh yale nayo yalikuwa makubwa mwenzenu aliyokuwa ananiletea kaka Imran. Heti nijaribishe kufuli halafu anione sasa ningeanzia wapi kusaula. Duniani kuna mauzauza jamani, nyie acheni muyasikie hivihivi kwa wengine.

“Wasema?” nikahoji kwa upole nikijifanya sikusikia maneno yake.

“Zijaribishe nione, au umevaa moja hapo?” alihgoji kaka Imran huku akipeleka mkono wake kutaka kufunua khanga niliyokuwa nimejifunga.

“Aah kaka wacha!” nilizungumza kwa sauti ya chini huku nikiushika ule mkono wake uliokuwa ukielekea kusiko kuwa kunafahamika.

“Kama umevaa si unioneshe tu kidogo”

“Hapana”

“Hapana nini sasa?”

“Sijavaa”

“Kwahiyo hapo hujavaa kitu”

“Abee”

“Hapo ulipo hujavaa kitu?”

“Nime…si…nime….” Nikajikuta nikishindwa kujibu swali lake lile.

“Hujavaa” Kaka Imran akadakia.

“Nimevaa” Nikajibu kwa mkazo

“Hebu tuone kama kweli umevaa” Mnh kaka Imran alizungumza huku akipeleka mkono wake kwa haraka kwenye madafu yangu ya nyuma




“Haya nambie na zile Chuchurichu nazo pia hujazipenda?”

“Mnh chuchurichu ndio nini?”

“Aah zile za ndani bwana!” alihoji kaka Imran swali amablo kwakweli sikuwa nimelitegemea hata kidogo. Nikabaki kimya nikitoa tabasanu pasipo kuzungumza neno lolote.

“Heti mtoto mzuri, nijibu basi” Kaka Imrani alizungumza huku mkono wake wa kushoto akiwa ameupeleka kwenye kichogo changu na kupapasa nywele za shingoni.

“Nimezipenda” nilijibu huku nikibonyea chini kwa mshituko kutokana na kitendo cha kaka Imran kunitekenya nyuma ya shingo.

“Unaweza kuzijaribu namimi nione zilivyokupendeza?” kaka Imrani alizungumza kwa sauti ya chini zaidi ambayo ilikuwa kama vile ikinibembeleza.

Mnh yale nayo yalikuwa makubwa mwenzenu aliyokuwa ananiletea kaka Imran. Heti nijaribishe kufuli halafu anione sasa ningeanzia wapi kusaula. Duniani kuna mauzauza jamani, nyie acheni muyasikie hivihivi kwa wengine.

“Wasema?” nikahoji kwa upole nikijifanya sikusikia maneno yake.

“Zijaribishe nione, au umevaa moja hapo?” alihgoji kaka Imran huku akipeleka mkono wake kutaka kufunua khanga niliyokuwa nimejifunga.

“Aah kaka wacha!” nilizungumza kwa sauti ya chini huku nikiushika ule mkono wake uliokuwa ukielekea kusiko kuwa kunafahamika.

“Kama umevaa si unioneshe tu kidogo”

“Hapana”

“Hapana nini sasa?”

“Sijavaa”

“Kwahiyo hapo hujavaa kitu”

“Abee”

“Hapo ulipo hujavaa kitu?”

“Nime…si…nime….” Nikajikuta nikishindwa kujibu swali lake lile.

“Hujavaa” Kaka Imran akadakia.

“Nimevaa” Nikajibu kwa mkazo

“Hebu tuone kama kweli umevaa” Mnh kaka Imran alizungumza huku akipeleka mkono wake kwa haraka kwenye madafu yangu ya nyuma na kuyaminyaminya. Jamani nyie mjini kuna mambo!


ENDELEA

“Mamaaa!” Nilipiga kelele pasipo kujitambua kutokana na hali ambayo nilikuwa nikiihisi mwilini mwangu kutokana na kitendo cha kaka Imarani kunishika madafu yangu.

“Shsssss!” Kaka Imran alininyamazisha kwa wasiwasi mkubwa.

Hata mimi mwenyewe nikajikuta nikijishangaa na kuhofia juu ya kitendo ambacho nilikuwa nimekifanya. Kwa usiku kama ule kupiga kelele ilikuwani kitendo cha kushitua watu hasa kwa waliolala mle ndani.

“Nini sasa?” alihoji kaka Imran kwa wasiwasi huku makiwa ameniachia.

“Usinishike huku” nikamwambia kwa sauti ya chini huku nikiwa nimejawa na aibu tele mtoto wa kike.

“Sasa na wewe kuguswa kidogo tu unapiga kelele hivyo, je ukinaniliu kabisa?” Kaka Imran alizungumza huku akishika kitasa cha mlango kutaka kufungua na kuondoka maana alikwishaona balaa lilikuwa likimkaribia. Alinitazama kwa jicho la kukata tamaa huku akianza kuhisi ugumu katika jitihada za kula tunda la rohoni alilokuwa akilitamani tangu siku niliyokuwa nimeingia ndani mle.

“We Tumuuu” Ilisikika sauti ya mama ikiniita kutokea nje ya chumba changu.

Kaka Imran alishituka na kuachia kile kitasa cha mlango kwa wasiwasi, alinikazia jicho na kuweka kidole mdomoni kunionya nisizungumze chochote kwa mama.

“Tumuuu” sauti ya mama iliita tena baada ya kuona kimya kimetawala.

“Abee” nikaitika kwa sauti ndogo utafikiri nilikuwa kwenye usingizi mzito.

“Hebu fungua mlango” Mama alizungumza huku akiwa amekishika kitasa cha mlango wangu na kukinyonga. Kwakuwa sikuwa nimefunga mlango, mojakwamoja mama aliufungua na kuchungulia ndani. Kaka Imrani alikuwa amekwisha kimbia nyuma ya mlango na kujibanza. Na mimi nilisogea mlangoni na kujifanya nilikuwa nakwenda kumfungulia mama mlango.

“Vipi una tatizo gani?” alihoji mama kwa wasiwasi.

“Kwanini mama?” Nikahoji kama vile nilikuwa usingizini na sikujua kilichokuwa kimetokea.

“Mbona nimesikia unapiga kelele?”

“Mnh! Kelele? Hapana mama sio mimi” nilijifanya kushangazwa na taarifa zileza mama.

“Mwantumu, unajua nimekusikia kwa masikio yangu na wala sikuwa nimelala” mama alizungumza kwa umakini.

“Hapana mama labda nilikuwa naota” nikazungumza kwa kujiamini.

“Kweli?” Mama alihoji huku akiwa amenikazia macho usoni.

“Kweli mama” Nilijibu huku macho yangu nikiyapeleka pembeni.

“Haya funga mlango na uzime taa” Mama alizungumza na kuondoka.

Pale nyuma ya mlango kaka Imran alikuwa ameweka mikono yake kifuani huku akiomba Mungu mama yake asiingie chumbani mle. Alitoa pumzi ndefu na kusogea mlangoni. Alisikilizia kwa sekunde kadhaa kisha alipohakikisha kuwa mama yake alikuwa amekwisha kuingia chumbani kwake, nayeye alichomoka na kuingia chumbani kwake. Mtoto wa kike nilifunga mlango na kwenda kujitupa kitandani.

Vituko vya kaka Imran vilizidi kuufanya usiku wangu kuwa mgumu. Mawazo yalinizidia kwenye ubongo wangu. Nikakumbuka kauli ya kaka Imrani aliyosema kuwa kwasababu nilikuwa kitoto kidogo nanuka shombo hivyo angenila kwa ndimu na pilipili. Sasa nikaanza kuhisi ukweli wa kauli yake ile.

Hata hivyo katika mawazo yangu yale nilitamani sana ujio ule wa kaka Imran ungekuwa ni ujio wa Fadhili mwanaume ambaye ndiye pekee alikuwa ameukosha mtima wangu tangu nilipokuwa nimefika pale jijini Dar es Salaam. Zote hizo zilikuwa ni tamaa tu nisingeweza kubadilisha na kumfanya Imran kuwa Fadhili ingawa walikuwa ni mtu na kaka yake. Mawazo yaliendelea kunitinga hadi kwenye mida ya saa tisa na nusu hivi za usiku ndipo usingizi ukanichukua tena kwa kuniiba pasipo hata kujitambua.

****


Kichwa kilikuwa kizito sana kutokana na usingizi niliokuwa nao asubuhi ya siku hiyo. Inawezekana hali ile ilikuwa imetokana na kukosa usingizi kwa muda mrefu usiku uliopita mishemishe na kukuru kakara za kaka Imrani pamoja na mawazo yaliyokuwa yamenitawala.

Nilijipindua pale kitandani kwangu huku nikisikilizia sauti za majogoo zilivyokuwa zikipokelezana kuwika. Mara kadhaa niliinua shingo yangu kutazama mwanga wa jua kupitia dirishani na kuendelea kuuchapa usingizi mtoto wa kike.

Sauti ya mlango wa mama ukifunguliwa ilinigutusha na kunifanya nikurupuke mbio kutoka pale kitandani na kuvaa nguo haraka tayari kwa kutoka nje kuanza kazi za siku mpya.

“Tumuu” Sauti ya mama iliita kutokea nje ya chumba changu.

“Abee mama” niliitika haraka nikijifanya nilikuwa macho kwa muda mrefu.

“Vipi mama unaumwa?”

“Hapana mama” nilijibu huku nikiwa bado chumbani nikimalizia kufunga kiremba kichwani.

“Mbona leo umepitiliza?” mama naye akaendelea kuhoji akiwa nje.

“Hapana mama nimekwisha amka” nilijibu na kufungua mlango.

Nilimkuta mama amesimama mlangoni akiwa tayari amekwisha jiandaa tayari kwa kuondoka. Mhn kusema kweli mwenzenu nilijawa na aibu kwa kiasi kikubwa. Siku zote muda kama ule nilikuwa nimeshafanya usafi wa ndani na kuandaa kifungua kinywa kwasababu watu wote walikuwa wakienda kazini asubuhi.

“Shikamoo mama” nilisalimia kwa sauti ya chini.

“Marahaba, upo sawa wewe?” mama alihoji kwa sauti ya upendo.

“Ndio mama, nipo sawa”

“Una uhakika?” mama aliendelea kudadisi huku akiwa amenikazia macho usoni.

“Sina tatizo mama” nikajibu huku nikisugua sugua vidole vya mikono yangu.

“Haya mimi ndio naondoka, ilahakikisha baba yako haondoki bila kunywa chai sawa?” mama alizungumza kwa msisitizo.

“Sawa mama” nilijibu huku nikimfuata nyuma.

Tulipofika nje mama aliingia kwenye gari na kuliwasha tayari kwa kuondoka. Mimi nilielekea getini na kulifungua. Macho yangu yalikuwa yakitazama magari ambayo yalikuwa yamebakia nyumbani pale. Niliweza kuona gari la baba na gari la Fadhili tu, lakini gari la kaka Imran halikuwepo jambo ambalo lilinifanya nigundue kuwa alikuwa tayari amekwisha ondoka. Sikujisikia vizuri kwani ilikuwa ni kawaida yangu kuhakikisha watu wote ndani mle hawaondoki bila ya kunywa chai.

Mama alitoa gari kisha kama kawaida ya alipofika katikati ya geti alisimama na kushusha kioo.

“Tumuuu” aliniita.

Nilizunguuka na kumfuata kule kwenye dirisha la mlango wake. Alinitazama kwa sekunde kadhaa kisha akameza funda la mate.

“Leo umezembea, si unaona kaka yako Imran ameondoka pasipo kunywa chai?” mama alizungumza kwa sauti ya chini.

“Nisamehe mama sito rudia tena” nilizungumza kwa upole.

“Haya kaendelee na kazi” mama alizungumza na kuondoa gari kutoka pale getini. Nilifunga geti lile kisha haraka sana nikarejea ndani ambako nilielekea moja kwa moja jikoni kuandaa chai kwaa jili ya baba na Fadhili.

Wakati nipo jikoni nikikaanga mayai kwenye jiko la pembeni nikaweka sufuria iliyokuwa ikichemsha maziwa. Nilikuwa nikijitahidi kufanya maandalizi yale kwa haraka angalau nisiwe nimeharibu kabisa.

“Hodii” nilisikia sauti ya mtu akliita huku akigonga hodi kutokea nje. Nilisikiliza tena kwa makini pasipo kutoka.

“Tumuuu!” sauti ya mgongaji wa geti ilisikika ikilitaja jina langu.

Niliweka pembeni kijiko nilichokuwa nikigeuzia mayai na kutoka nje mbio kumsikiliza mtu ambaye alikuwa akibisha hodi kwa kuliita jina langu. Nilipofika nilimkuta Bupe Yule mama wa mgahawani amesimama na mkononi akiwa na dumu la lita tano lililokuwa limejaa juisi.

“Shikamoo” nilimsalimia huku nikilitazama lile dumu lake la juisi.

“Marahaba binti wa kitanga, habari ya weye" Mama Yule alizungumza kwa kuiga lafudhi ya kitanga.

“Salama karibu”

“Mdogowangu hebu niwekee hii juisi yangu kwenye friji, naona lakwangu leo limegoma kuwaka kabisa” alizungumza Bupe huku akinikabidhi kale kagalani kalikokuwa kamejaa juisi ya parachichi. Niliipokea galani ile pasipo kuzungumza neno lolote na kuondoka nayo.

Sikuweza kuamini macho yangu kwa kile ambacho nilikuwa nimekikuta jikoni baada ya kurejea. Maziwa yalikuwa yamefurika na kumwagika yote, mayai nayo nilikuwa nimeyaacha jikoni hivyo nikayakuta yameungua kabisa na kuwa meusiii kama mkaa. Yaani mtoto wa watu wa kitanga nikachanganyikiwa.

Nilizima jiko haraka na kuepua ile flampeni ya mayai iliyokuwa jikoni. Nilishusha sufuria ya maziwa na kuiweka pembeni ikiwa imesalia na maziwa ambayo hayakuweza kujaa hata kikombe kimoja. Nilichukua kitambaa na kuanza kufuta maziwa yaliyokuwa yamemwagigia juu ya jiko huku nikiwa natetemeka kwa woga na wasiwasi.

“Hujambo binti” Ilikuwa ni sauti ya baba iliyonisalimia kutokea nyuma. Niligeuka haraka sana na kumkuta amebeba brifkesi yake mkononi tayari kwa kuondoka. Jamani jamani Mungu huyu, yani siku ikiwa ya mikosi ni mikosi tu. Sijui hata kulikuwa kumeingia ibilisi gani katika ajira yangu.

“Shikamoo baba” nilimsalimia mzee Sekiza kwa heshima zote zilizokuwa zimechanganyikana na woga.

“Marahaba hujambo”

“Sijambo baba”

“Chai vipi mbona meza leo imenuna?”

“Chai?” nikahoji kama vile nilikuwa sikusikia alichohoji.

“Ndio chai, kwani wewe hujui jukumu lako la kila asubuhi?” baba alihoji kwa kuonekana wazi hakuwa amefurahishwa na kitendo changu cha kuchelewa kuandaa chai siku hiyo.

“Naomba unisamehe baba sitarudia tena” nilizungumza kwa upole huku mikono yangu nikiwa nimeikumbatia kifuani kama ishara ya kuomba msamaha. Alinitazama kwa sekunde kadhaa na mwisho akaonekana kunielewa.

“Mimi naondoka ila kaka yako yupo, hakikisha anakunywa chai. Mimi naona nimechelewa kazini” Baba alizungumza huku akitazama saa yake ya mkononi. Sikuwa na cha kuzungumza chochote kupinga kauli ya baba na amri yake. Hata hivyo moyoni mwangu niliumia na kuogopa sana kwasababu mama alipoondoka asubuhi alinisisitizia kuhakikisha baba anakunywa chai ndipo aondoke.

Baba aliondoka na kunifanya na mimi nimfuate nyuma kwaajili ya kwenda kufungua geti. Aliingia kwenye gari yake na kutoka pasipo kuzungumza kitu chochote kama ambavyo ilikuwa kawaida yake kila siku nilipokuwa nikimfungulia geti. Alipotoka tu nikafunga geti na kurejea ndani mbio.

“We mama wa kitanga!” nilipoingia ndani tu nikasikia sauti ya Fadhili ikiita kutokea sebleni. Nilishituka sana lakini nikauchuna kama vile sikuwa nimesikia sauti ile.

“We bi dada!” Fadhili aliita tena. Niliendelea kuuchuna kama vile sikuwepo ndani ya nyumba ile, kumbe nilikuwa nikiendelea kufanya usafi harakahara kwenye jiko lililokuwa limemwagikiwa na maziwa.

“Mwantumu!” Safari hii akaongeza sauti.

“Abee” nikaitia huku nikiwa bado nipo jikoni nikimalizia kufuta futa.

“Njaa mama njaa. Lete mavituzi hayo tupige sie tuondoke, au leo unataka tubaki sote hapa home?” Fadhili alizungumza kwa masihara kama ilivyokuwa kawaida yake. Masikini ya Mungu laitani angejua kuwa huko jikoni kulikuwa kumeharibika wala asingelikaa akalisubilia msosi. Mtoto wa kike nikajikausha kama vile sikumsikia.

“We mama we unaua hukuuu! Hebu nionee huruma kijana mwenzio” Fadhili aliendelea kuleta masihara yake pale sebleni. Maneno yake yale yalinifanya niangue kicheko kwa sauti ya chini huku nikiwa nimeziba mdomo kujizuia kucheka kwa sauti.

“Aaaaaah!” Fadhili alipia miayo kwa sauti kubwa heti kunifahamisha kuwa alikuwa na njaa. Masikini ya mungu mtoto wawatu wa bosi nilimuonea huruma ingawa alikuwa akinivunja mbavu kule jikoni kwa vituko vyake.

Nilichukua sufuria nyingine ndogo na kubandika maji haraka jikoni kwa lengo la kumchemshia chai ya rangi mtoto wa watu ili kibarua changu kisije kuota nyasi buree.

“Haaaa!” sauti ya Fadhili ilinigutusha sana. Alikuwa amesimama kwenye mlango wa kuingilia jikoni na kuhamaki aliponiona ndio nakukuruka kuinjika sufuria ya chai jikoni. Niligeuka na kumtazama huku nikionekana wazi kuwa nilikuwa nikmeshituka.

“Kwahiyo haya ndiyo yaleee mambo ya kitanga yanayosifika?” Fadhili alihoji mara tu nilipomgeukia.

“Mambo gani jamani?” nilihoji huku nikijitahidi kuvaa tabasamu japo la kubandika.

“Ya kunyweshana chai saa sita za mchana”

“Yaani kaka Fadhili we acha tu” nilizungumza kwa sauti ya chini.

“Niache nini wakati mwenzio unanipeleka kazini bila kula” Fadhili alizungumza kwa sauti yake ambayo haikuwa inafahamika kama ni ya kukasirika ama ni ya masihara kwa vile ambavyo hakuwa mtu wa kupenda kununa nuna kama alivyokuwa kaka Imran.

“Yaani yaliyonikuta leo nashindwa hata kuelezea”

“Mangapi?”

“Wacha masihara kaka Fadhili wewe”

“Sasa si uzungumze, mi nitajuaje”

“Mwenzio leo nimeunguza mayai, na chai yote imemwagika jikoni”

“Ulikuwa unasinzia?”

“Si afadhali ningekuwa nasinzia”

“Kumbe ulilala kabisa?”

“Sikiliza basi”

“Hakuna cha kusikiliza wewe umezidisha mawazo, mtoto mdogooo mawazo lukuki. Ona sasa umenishindisha na njaa mtoto wa mwanamke wa kitanga mwenzio” alisema kaka Fadhili huku akitabasamu.

“Basi nisamehe” nikazungumza kwa sauti ya kudeka.

“Adhabu yako….”

“Enhe…”

“Leo mchana sirudi, utakula peke yako lunch”

“Aaah usifanye hivyo kaka Fadhili mwenzio kula bila ya wewe siwezi” nikazidi kudeka mtoto wa kike.

“Utajiju” Fadhili naye akajifanya amenuna.

“Basi nambie nikufanyie nini ili urudi” nikajizungungumzisha huku nikijichekesha chekesha

“Nipikie chai ya madhiwa” Fadhili alizungumza kwa lafudhi ya kitoto maneno yale ilhali akifahamu maziwa siku ile hayakuwepo mengi na hayo machache yenyewe yalikuwa yamemwagika yote jikoni.

“Maziwa yamemwagika yote jikoni” nikazungumza kwa kubembeleza.

“Thatha mimi nitafanyaje?” alihoji kwa lafudhi yake ya kitoto kuonesha deko.

“Basi nikupe haya yakwangu unyonye” nikazungumza huku nikiwa nimeshika madafu yangu ya kifuani.

“Thitaki hayo mimi, nataka ya ngo’mbe”

“Kumbe we hujui tu, haya matamu kuliko hata hayo ya ngo’mbe” mtoto wa kike nikazungumza kwa ile sauti yangu ya kubana.

“Kwanza viziwa vyenyewe hivyo havina kitu chochote” Fadhili alizungumza huku akikwepesha macho yake kuhofia kutazama kifuani kwangu ambako kulikuwa na madafu yaliyokuwa yametuna ipasavyo kiasi cha kumfanya mwanaume yeyote asiye na kasoro kuyatamani.

“Si uonje uone kama hayana kitu!” nilizungumza huku nikimsogelea na kufungua vishikizo vya gauni langu vilivyokuwa kifuani. Nilimshuhudia Fadhili macho yakimtoka utafikiri alikuwa ameona kitu fulani cha ajabu sana hapa ulimwenguni. Sikuweza kufahamu ni kwa namna gani niliweza kupata ujasiri wa namna ile mbele ya mwanaume Yule.

Akiwa bado ameshangaa tayari sidiria yangu nyeupe iliyokuwa na kitambaa cha resi ilikamatwa vyema na mikono yangu tayari kwa kumtolea kile ambacho nilikuwa nimekikusudia. Ndio, nilikuwa namtamani sana Fadhili kiasi cha kusisimkwa mwili kila nilipokuwa namuona.



ENDELEA….


“No! Tumu….usi…usi….ahsante” Fadhili alizunguza kwa kigugumizi na kuondoka pasipo hata kuaga.


Nilibakia jikoni pale nimesimama huku mikono yangu ikiwa imekamata gauni langu lililokuwa wazi maeneo ya kifuani. Nilign’ata meno yangu ya chini kwa hasira na kuelekea chumbani kwangu. Sikutamani hata kwenda kumfungulia geti. Nikaona mwanaume gani yule ambaye ukimtega kwa urimbo anajinasua kwa fimbo na ukimtega kwa mambo anajinasua kwa jambo. Nikajitupa kitandani kwa hasira. “Hivi ni kwanini Fadhili ananidharau mimi, au ananiona katoto kadogo kama alivyozungumza usiku? Mbona kaka Imrani alikuwa akionekana wazi kuvutiwa na mimi pamoja na kwamba sikuwahi kumuonesha kumtaka? Au Fadhili ni mgonjwa?” nikajiuliza maneno mengi nikiwa pale kitandani.


****


Nikiwa kitandani nikajikuta usingizi ukinichukua na kulala fofofo masikini mtoto wa watu mie. Basi nilipiga mbonji hadi kwenye mida ya saa nane hivi ndipo nilipokurupuka na kutoka chumbani kwangu mbio kama mwizi. Haraka sana macho yangu yalitua kwenye saa ya ukutani ambapo ndipo nilipobaini kuwa ilikuwa ni saa nane za mchana.


“Mtume simama!” nilishituka na kuweka mkono wangu kifuani kama vile nilikuwa najipima mapigo ya moyo. Niliingia jikoni haraka sana na kuanza kufungua makabati ya vyakula ili niweze kupika. Akilini mwangu nilikuwa namuwaza sana Fadhili kwani ni yeye pekeyake ambaye alikuwa na kawaida ya kurudi nyumbani mchana kwaajili ya chakula.


“Hodiii” sauti ya mtu kutiokea nje ya geti ilisikika ikiambatana na sauti ya kugongwa kwa geti hilo. Moyo wangu ukashituka kidogo nikiamini kuwa mgongaji alikuwa ni Fadhili.


“Mungu wangu! Haya yote yanatokea wapi, mbona nimekuwa mzembe kiasi hiki leo?” Nilitoka nje na kuchungulia kwenye tundu dogo la pale getini. Moyo wangu ulipata ahuweni baada ya kumuona mgongaji alikuwa ni dada Bupe yule mama muuza mgahawa wa jirani. Nilifungua geti na kuchungulia nje kumkaribisha Bupe.


“Karibu dada” nikamkaribisha.


“Ahsante mwaya, weye wa lala weye?” mama yule alizungumza huku akijitahidi kuiga lafudhi yangu ya kitanga ingawa hakuwa anaimudu.


“Hapana sikuwa nimelala”


“Kumbe wafanyaje weye?”


“Nilikuwa napika” nikajibu kwa ufupi kwasababu sikuwa nimefurahishwa na viswali vyake vilivyokuwa vikinigusa.


“He! Saa hizi wapika! chakula cha jioni?”


“Hapana napika chakula cha mchana” nikamwambia.


“Kwanini sasa umechelewa hivyo?”


“Nilikuwa nimepitiwa na usingizi”


“Kwahiyo ndo waamka hivyo?” alihoji nami nikaitikia kwa kichwa.


“Sasa unapika nini”


“Nataka kupika nyama na ugali”


“Unataka kupika ama ndio unapika?”


“Nataka kupika”


“He! Makubwa mwaya, kwahiyo ndo mambo ya kitanga hayo?” mama yule akahoji swali la kishambenga ambalo lilinikera ile mbaya. Hata hivyo nikajikaza kuto kumuonesha kuwa nilikuwa nimekasirika.


“Karibu dada Bupe” nikamkaribisha kwa msisitizo baada ya kuona anaingilia mambo ambayo hayakuwa yakimhusu. Halafu nilikuwa naona akizidi kunipotezea muda zaidi ambao pengine ningeutumia kumuandalia Fadhili chakula.


“Sikiliza mdogo wangu, mie kule nimekwisha pika. Twende ukachukue chakula umuekee kakaako” mama yule alizungumza. Moyo wangu ulisita kwa kuhofia kuleta chakula cha hotelini nyumbani wakati ndani kulikuwa na kila kitu.


“Usiogope mdogowangu, we unahifadhi vizuri kwenye poti hata yeye akija hawezi kuelewa kama umechukua mgahawani” alisema mama yule maneno ambayo kwa kiasi fulani nilihisi yakiniingia akilini.


“Kweli dada?”


“Nenda ukalete hotipoti”


“lakini dada wewe….”


“Hakuna cha lakini bwana weye, nenda ukalete poti hukoo” dada Bupe alizungumza huku akinisukuma kwa mkono wake wa kushoto kuelekea ndani. Sikubisha hata kidogo, niliondoka haraka kuelekea ndani.


“Lete na dumu langu la juisi” alinambia dada Bupe kwa sauti wakati naingia ndani.


“Sawa” Nilijibu na kuzama ndani.


Nilipotoka na hotipoti zangu mbili mkononi sikumkuta dada Bupe pale getini. Sikupata shida sana ya kumtafuta wala kushangaa kwa kile kilichotokea. Nilitoka haraka getini na kwenda hadi mgahawani kwake. Nilimkuta akigeuza wali jikoni.


‘Hodiii” nilibisha hodi nilipokuwa naingia mgahwani mle.


“Karibuuu” dada Bupe akaniitikia kwa bashasha.


Nilipitiliza moja kwa moja hadi jikoni na kuketi kwenye kiti kidogo kilichokuwa pembeni ya jiko alilokuwa anapikia. Alipokea Hotipoti moja na kujaza ugali.


“Haa dada Bupe punguza huwo mwingi sana” nikasema


“Wacha machachari wewe kwani tumbo ni lako” akanambia huku akifunika hotipoti lile na kupokea hotipoti la mboga na kunikabidhi lile la ugali. Alifunua chungu cha nyama na kuniwekea kisha akafunika na kunikabidhi.


“Haya peleka haraka”


“Asante dada Bupe” nilijibu huku nikijiinua kutoka pale kwenye kiti.


“Nenda urudi ninashida na wewe” dada Bupe alipaza sauti wakati nilipkuwa natoka.


Nilitembea kwa haraka sana na kuingia getini pasipo kuonekana na mtu yeyote kama nilikuwa nimebeba chakula kutoka mgahawani kwa dada Bupe. Jamani kuna watu wana roho nzuri nyie, sikuweza kuamini kama mwanamke yule niliyekuwa namchukia ndiye aliyeweza kunisaidia kutoka kwenye majaribu ya siku hiyo.


Niliandaa chakula kile mezani haraka kisha nikakumbuka wito wa dada Bupe, nilitoka na kuelekea mgahawani.


****


Nilipofika mgahawani pale dada Bupe alikuwa ameniwekea chakula kwenye sahani na kunikabidhi mara tu nilipofika.


“Haya nawewe ule” Akazungumza mwanamke yule alipokuwa akinikabidhi sahani ya chakula.


“Mnh dada wewe mkarimu” nikazungumza huku nikipokea.


“Wacha maneno mengi hebu kula huko” akanambia huku akisuuza sahani haraka haraka.


Mwenzangu nikaanza kula taratibu kama vile sikuwa mimi. Nilete utani kwenye maswala ya msosi, nani kasema? Nikapiga msosi ule hadi nikamaliza.


Dada Bupe alikuwa ameketi kwenye kistuli alichokuwa amekilaza kwa pembeni akiosha vyombo. Mimi nilikuwa nimeketi kwenye kiti cha plastiki kilichokuwa pembeni yake nikichambua njegere za biashara. Nikakumbuka kitu na kuona si vibaya kumuyomba ushauri.


“Dada” niliita


“Mdogo wangu” aliitika pasipo kunitazama huku akisugua birauli.


ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

BLOG