Search This Blog

Sunday, April 18, 2021

HOUSEGIRL WA KITANGA (2) - 5

   


Chombezo : Housegirl Wa Kitanga (2)

Sehemu Ya Tano (5)




“Umeshaanza ufirauni wako, tamaa za kimwili zitakuua we mzee” mama alizungumza kwa hasira.

“Najua unampendana sana na huyu mtoto na ndiyomaana nimeona nimuoe ili mzidi kupendana zaidi” Baba alizungumza kwa unyenyekevu.

“Huoni hata aibu, mwenyewe unamuita mtoto halafu bado unataka kujishusha kwake” mama alizungumza.

“Hapana mke wangu sijishushi, bali yeye ndio nampandisha” alizungumza mzee Sekiza kwa msisitizo.

“Niondolee laana zako hapa, mwanaume gani wewe usiye na aibu hata chembe” mama alizungumza kwa hasira.

“Ndio utajua sasa, dawa yako ni ndogo tu. Lazima nimuoe Mwantumu!” Baba alizungumza na kujilaza huku akiwa na hasira baada ya mama kupinga wazo lake la kuongeza mke wa pili.

Baba alilala pale kitandani lakini mawazo yake yote yalikuwa juu yangu mimi na lile vazi langu la kanga moja nililokuwa nimelivaa siku ile nilipokuwa nikisugua zulia. Alitamani sana kama angekuwa ameshanishawishi ili atoke na kuja kunikumbatia lakini ilishindikana kwasababu binti mwenyewe sikuwa hata na tetesi ya kilichokuwa kikiendelea kichwani mwake.

*****

Miongoni mwa wanaume ambao walikuwa wameingia kwenye mkumbo wa kulisaka penzi langu alikuwa ni pamoja na kija Shebughe. Kijana yule aliyekuwa akijitambulisha kwa jina la Sheby. Ni yule kijana ambaye alikuja nyumbani na kaka Imran na kumtambulisha kwangu kama rafiki yake.

Kijana Sheby ndio huyo huyo kijana ambaye nilikaa naye siti ya jirani siku nilipokuwa nikisafiri kurudi kijijini kwetu Tanganyika. Na ndiye huyo ambaye nilimsukumia zigo la uchumba siku ambayo Imran alikuwa amefunga safari kuja Tanga kutaka familia yake ikamtolee posa nyumbani kwetu.

Shebughe alikuwa amejiinamia na mikono ameiweka kichwani huku akihisi hali isiyo eleweka katika mishipa yake. Viungo vya mwili vilinyongo’onyea na kuhisi kushindwa kufanya jambo lolote lile. Chakula kilikuwa hakipiti katika kinywa chake kama ilivyokuwa kawaida.

Kwa bahati mbaya au nzuri Shebughe alikuwa amepanga kwenye nyumba ya Dada Bupe kule Kijitonyama tulipokuwa tukiishi mimi na mama kabla ya kurudi kwenye nyumba ya Mabibo Hosteli. Bupe huyo alikuwa ni yule dada Bupe ambaye alikuwa akinikuwadia kwa wanaume na matokeo yake akaishia kuunguzwa na mafuta ya kupikia usoni kwa sababu ya hiyo tabia yake ya kukuwadia wasichana kwa wanaume.

“Sheby..” sauti ya mwanamke ilimgutusha Shebughe kutoka pale alipokuwa amejiinamia na kumuangalia mtu ambaye alimuita.

“Vipi sikumbili hizi haupo sawa mdogo wangu, una tatizo gani?” mwanamke yule alikuwa ni dada Bupe.

“Dah sister nahisi sipo sawa kabisa” Shebughe alizungumza kwa sauti ya uchovu.

“Unaumwa nini?” Dada Bupe alihoji.

“Hata sielewi”

“Mdogo wangu, ugonjwa wako nahisi ninaufahamu vizuri sana” mwanamke yule alizungumza kwa kujiamini.

Shebughe aliinua macho yake na kumtazama Dada Bupe usoni kisha akaachia tabasamu la kukata tamaa.

“Usidharau Sheby, naweza nikakusaidia kama ukiwa muwazi” alizungumza dada Bupe huku akiketi pembeni mwa Shebughe.

“Acha utani basi dada Bupe. Hakuna mtu anayeweza kutatua tatizo langu zaidi ya mimi mwenyewe” alizungumza Shebughe kwa msisitizo.

“Kuna msichana anasumbua mtima wako, uwongo?” alihoji dada Bupe kwa umakini mkubwa.

“Wewe umejuaje dada Bupe?” Shebughe akahoji kwa mshangao.

“Dalili za huo ugonjwa zinaonekana kwako kwa asilimia 99” dada yule alizungumza kwa kujiamini.

“Dalili zake ni zipi?” Shebughe akahoji kwa umakini mkubwa baada ya kuhisi mwanamke yule angeweza kuwa msaada kwake hata wa mawazo.

“Kwanza kabisa unapoteza hamu ya kula, kuzungumza na watu, kutembea, mwili huchoka, unapoteza uwezo wa kufanya shughuli zako za kila siku, unatamani kulala muda wote lakini hupati usingizi na hujikuta ni mtu mwenye hasira zisizo na sababu mara kwa mara” alizungumza dada Bupe kwa ufasaha.

“Upo sahihi dada Bupe, unafikiri nitumie dawa gani ili kuondokana na ugonjwa huu?” Shebughe akahoji kwa umakini.

“Matibabu pekee ya ugonjwa huo ni kuhakikisha unafanikiwa kile kinachokutatiza” alizungumza dada Bupe kwa msisitizo.

“Na kama nisipofanikiwa itakuwaje?”

“Usipofanikiwa maana yake utaugua ugonjwa huo kwa muda mrefu hadi pale utakapompata msichana ambaye utampenda kwa dahati kuliko huyo anayekusumbua, vinginevyo utaugua milele” alizungumza dada Bupe kwa umakini.

“Dada Bupe nampenda sana yule msichana lakini sioni dalili yoyote ile ya kumpata” Shebughe alizungumza kwa hisia kali kiasi cha kumgusa dada Bupe.

“Yeye anafahamu kama unampenda?” Bupe alihoji.

“Sijui lakini nilikwishawahi kumueleza hisia zangu”

“Mara ngapi?”

“Kama mara mbili hivi” Shebughe alieleza.

“Na yeye amekujibu nini?”

“Kwakweli simuelewi, hajawahi kuniambia ndio wala hapana”

“Sasa kwanini unakufa kihoro ilhali nafasi bado unayo?” dada Bupe akazungumza kwa msisitizo.

Shebughe aliinua macho na kumtazama dada Bupe usoni kisha akameza funda la mate mazito. Alivuta pumzi na kuziachia kwa kuzisukuma nje kwa nguvu.

“Dada Bupe, tatizo ni kwamba rafiki yangu ameshanitambulisha kuwa anataka kufunga ndoa na huyo mrembo!” Shebughe alizungumza kwa msisitizo lakini kwa sauti iliyokata tamaa.

Dada Bupe alivuta pumzi na kuziachia kisha akajikuna kichwa kama vile alikuwa anatafakari maelezo ya Shebughe.

“Duh kweli hilo ni tatizo!” alizungumza dada Bupe kwa sauti ya kukata tamaa.

“Umeona mwenyewe balaa hilo?”

“Kwani wewe na huyo rafiki yako ni nani aliyeanza kumuona huyo binti?” alihoji Bupe.

“Kwa kweli sielewi, lakini wakati natambulishwa nilikuwa tayari nimeshamueleza hisia zangu yule binti” Shebughe alizidi kutoa maelezo.

“Huyo rafiki yako anafahamu kama na wewe ulishawahi kumtongoza huyo binti?” alihoji Bupe.

“Hajawahi kufahamu” alijibu Shebughe kwa sauti ya unyonge.

“Sasa kwasababu yeye ametangulia kukutambulisha unaonaje ukaachana naye?” Bupe alitoa wazo.

“Namuachaje kwa mfano!” alizungumza Shebughe kwa msisitizo.

“Duh vita vya mapenzi unaviweza lakini mdogo wangu?” Bupe akahoji kwa msisitizo.

“Nitapambana dada Bupe, Sipo tayari kumpoteza binti yule kirahisi rahisi hivi?” Shebughe alizungumza kwa msisitizo.



“Huyo binti ni wa wapi?” Bupe alihoji.

“Ni mtoto wa kitanga!”

“Na hilo ndilo tatizo, nyie watu wa Tanga huwa kwenye mapenzi utafikiri mmerogewa nayo!” alisema dada Bupe.

“Tatizo lako unapenda utani mno, hata kwenye mambo ya msingi we unaleta masihara” Shebughe alilalamika.

“Ingekuwa ni enzi zangu, ningepambana kwa kadri niwezavyo kuhakikisha nalitatua suala lako” Bupe alizungumza kwa kujitapa na majigambo.

“Kama unaweza naomba unisaidie dada Bupe” Shebuhe alisihi.

“Mnh! Huyo binti anaishi wapi?” dada Bupe alihoji.

“Mabibo Hostel”

“Wapi?” dada Bupe alihoji kwa mshituko.

“Mabibo”

“Anaitwa nani?”

“Ndwadwa…” Shebughe alijibu kwa msisitizo.

“Na huyo rafiki yako anaitwa nani?”

“Imran…”

“Imran Sekiza, sivyo?”dada Bupe akahoji kwa msisitizo.

“Kumbe unamfahamu?”

“Zaidi ya unavyomfahamu wewe” dada Bupe alizungumza kwa kujiamini.

“Kale kabinti ni kasichana kao ka kazi” Shebughe alijaribu kufafanua.

Maelezo ya Shebughe yalimfanya dada Bupe kushituka kidogo na kukumbuka siku ambayo nilimtoroka kaka Imran siku ile tulipokutana kule Kijitonyama nilipokwenda kumwaga takataka.

“Umesema huyo binti anaitwa nani?” dada Bupe alihoji kwa msisitizo mkubwa.

“Mwenyewe anajiita Ndwadwa lakini Imran anamuita Mwantumu” alieleza Shebughe.

“Kudadadeki! Huyo ni Tumu!” alizungumza dada Bupe kwa msisitizo huku akionekana kunifahamu vizuri sana.

“Vipi unamfahamu?” alihoji Shebughe kwa hamasa kubwa.

“Ni mdogo wangu na nimeishi naye kwa muda mrefu sana” dada Bupe alizungumza kwa msisitizo.

“Unasemaje, kwahiyo mambo yamekuwa marahisi sivyo?”

“Sio kama unavyofikiria, yule binti ni hatari mno”

“Unataka kusema nini dada Bupe?”

“Tumu ndiye aliyesababisha sura yangu kuungua na kuwa hivi” alizungumza dada Bupe kwa uchungu mkubwa.

“Unamaanisha nini?”

“Ni hadithi ndefu, lakini kilikuwa ni kama kisa chako” alizungumza dada Bupe na kumeza funda la mate.

“Ilikuwaje?” Shebughe akahoji kwa hamasa.

“Kuna wanaume walikuwa wanamgombania huyo Mwantumu. Kijana mmoja alichukua mafuta ya kupikia kutoka jikoni na kutaka kummwagia mwenzake, kwa bahati mbaya mafuta yote yakanirukia mimi usoni na kunifanya leo hii kuwa hivi” Dada Bupe alizungumza kwa uchungu mkubwa kiasi cha kudondosha machozi.

“Basi dada Bupe, kama mambo yenyewe ndio hivyo mimi basi! Sihitaji tena msaada wako dada Bupe” Shebughe akazungumza kwa hofu.

“Hapana mdogo wangu Sheby, nitakusaidia kwa kadri ya uwezo wangu. Yule dogo mimi ninammudu” dada Bupe alizungumza maneno yaliyoonekana kumtia faraja Shebughe.

“Nitashukuru sana dada Bupe, nampenda sana Ndwadwa mimi” Shebughe alizungumza kwa hisia.

“Tatizo ni kwamba huyo Imran sipatani naye kabisa. Niliwahi kuwa na mahusiano naye miaka mingi iliyopita” alizungumza dada Bupe.

“He kumbe!”

“Nilikuwa nampenda sana lakini tulihitilafiana kwasababu ya tabia yake ya umalaya” Bupe akaeleza.

“Duh pole sana”

“Itabidi nimshawishi turudiane ili wewe upate nafasi” Bupe alizungumza.

“Mi nakuaminia dada Bupe, fanya mambo bwana"

“Usijali, nitakuletea Ndwadwa wako” alizungumza dada Bupe na kujiinua kutoka pale alipokuwa ameketi na kuvuta hatua kuondoka huku akimuacha Shebughe akiwa na matumaini ya kulinasa penzi langu.

******

Kitendo kile cha kujibishana na dada Mainaya na kukataa simu aliyokuwa amepewa na kaka Imran kuniletea kiliwatia mashaka wawili wale na kuhisi kulikuwa na kitu kilichokuwa kiki endelea kati yangu na Fadhili.

Dada Mainaya alimueleza kaka Imran kuwa sababu ya mimi kumkataa alikuwa ni Fadhili. Ugumu wote ule niliokuwa nauweka ni kutokana na Fadhili. Hivyo Fadhili ndiye aliyekuwa ameonekana kuwa kikwazo kikubwa katika mkakatia wa kaka Imran kulinasa penzi langu.

Dada Mainaya na kaka Imran walijaribu kuumiza vichwa na kufanikiwa kuweka mikakati ambayo wao waliamini kwa kuitumia wangefanikiwa kuninasa nakumuweka pembeni Fadhili wangu ambaye kwa wakati huo tayari nilishaamua kumpenda.

Kutokana na mipango pamoja na mbinu za dada Mainaya, kaka Imran aliamua kufanya mazungumzo na wazazi wake ili kuona kama angeweza kuweka mambo sawa mapema iwezekanavyo.

Kikao kile cha dharura kilifanyika palepale Mabimo kwenye maeneo ya jirani na nyumbani na kiliwahusisha watu wane yani Kaka Imrana mwenyewe, Baba mzee Sekiza, mama Bi. Fatma na Binamu Mainaya.

“Baba na Mama pamoja na dada Mainaya” alizungumza kaka Imran na kumeza funda lamate.

“Tunakusikiliza” mama alijibu na baba pamoja na Mainaya wakaitika kwa vichwa kuungana na kauli ya mama.

“Mimi mtoto wenu nafikiri nimekua sasa”

“Tumefurahi kama umelitambua hilo” Baba alisema.

“Hakika umekua baba” mama naye akakazia.

“Sasa mtoto wenu nataka kupata jiko” kaka Imran alizungumza.

“Woow, hongera sana kaka” Mainaya alizungumza kwa furaha huku akiinua kinywaji juu na kupiga funda kwa ishara ya kuunga mkono wazo la kaka Imran.

Wote baba pamoja na mama nao pia walishindwa kuzuia furaha zao na kupiga makofi kutokana na taarifa njema kutoka kwa kijana wao. Walifurahi sana kwa maana ni ngumu mno kumkuta kijana kama kaka Imran awe na wazo la kufunga ndoa. Vijana wengi hawana mpango wa kufunga ndoa hadi itokee bahati mbaya binti amepata ujauzito asusiwe ndio aseme ameoa.

“Hivyo wazazi wangu, naombeni Baraka zenu kwa hili” kaka Imran alizungumza kwa heshima kubwa.

“Mwanangu tunakupatia Baraka zote tukiwa na mioyo myeupee!” baba alizungumza kwa msisitizo.

“Kila mlango wa mafanikio ufunguke kwa upande wako mwanangu” mama alizungumza kwa roho safi kabisa bila ya hata kinyongo.

“Unajua swala la kuoa ni jambo jema sana, hata ikitokea unapata uwezo wa kumiliki wake wawili, mimi nipo radhi kabisa” baba alizungumza kwa msisitizo akikumbushia lile ombi lake la kuongeza mke wa pili.

“Usimpotoshe mtoto mume wangu, maisha ya siku hizi hayasadifu mambo ya ndoa za mitara” mama alizungumza kwa umakini mkubwa.

“Lakini dini inakubali” baba alisema.

“Achana na baba yako mwanangu, tuendelee na mazungumzo yetu. Huyo mkwe wetu ni mwenyeji wa wapi?” mama alizungumza na kumalizia na swali la msingi sana kwa kaka Imran.

“Mama mimi ni mtu wa Tanga, lazima nikachukue chombo huko huko Tanga” kaka Imran alizungumza kwa msisitizo.

“Unasema anatokea wapi?” mzee Sekiza akajikuta akihoji kwa mshituko baada ya kusikia maelezo yale ya kaka Imran.

“Mbona unashituka kuna shida yoyote kuoa Tanga?” mama akahoji huku akianza kuhisi kitu.

“Hapana nataka kufahamu tu, maana asije akaoa ndugu zake huko” baba alizungumza kwa lengo la kubaraguza kile kitendo cha mshituko alichokionesha waziwazi bila ya kujificha.

“Kama umepandikiza mbegu zako huko utajua mwenyewe” mama alizungumza kwa upole kama vile anajilazimisha lakini ndio likuwa amelitoa lake la moyoni.

“Imran endelea mwanangu” alisema baba.

Kaka Imran akatazamana na Mainaya kisha wakakonyezana huku kila mmoja akionekana kuwa na hamasa kubwa ya kufahamu hatma ya mbinu ile waliyokuwa wameitumia.

“Mama na Baba, mimi mtoto wenu nimeamua kumuoa MWANTUMU” alizungumza kaka Imran kwa msisitizo mkubwa.

“Unasemaje wewe?” baba alihoji kwa kuhamaki kiasi cha kusimama pale alipokuwa ameketi.

“Tulia basi mtoto aeleze, mbona unakuwa hivyo mume wangu?” mama alizungumza kwa upole huku na yeye akiwa ameshituka kwasababu hakutegemea jibu lile.

“Huyo Mwantumu ni yupi baba?” mama alihoji kwa umakini huku akitegemea jibu tofauti kwasababu tayari Fadhili alikwisha mueleza mpangowake wa kufunga ndoa na mimi.

“Mimi namuongelea Mwantumu yule tunayeishi naye nyumbani” kaka Imran alizungumza taratibu.




“Hiyo ndoa haipo!” baba alijikuta akizungumza kwa kuhamaki.

“Kwanini isiwepo?” mama naye akahoji kwa msisitizo baada ya kumuona baba amepagawa kutokana na taarifa ile.

“Itawezekanaje sasa?” baba aliendelea kupagawa bila y ahata aibu.

“Kwanini isiwezekane!” mama akahoji kwa jazba.

“Nimesema huwezi kumuoa Mwantumu!” baba alisisitiza.

“Nimesema atamuoa Mwantumu!” mama naye alisisitiza.

“Tuone sasa!” alizungumza baba kwa jazba.

Tabia ya baba ilimfanya mama kuunga mkono suala lile bila hata kufikiri mara mbili kuwa Fadhili naye aliwahi kumuelezea mpango wake wa kutaka kufunga ndoa na mimi.

“Kwani Mjomba tatizo liko wapi?” Mainaya akaingilia kati na kuhoji.

“Tatizo! Inamaana we huoni tatizo?” baba alizungumza kwa hasira huku akitetemeka.

“Mimi bado sijaelewa mjue!” alizungumza kaka Imran kwa mshangao.

“Baba yako atakuwa analo lake jambo, mwambieni afunguke tumsaidie” Mama alizungumza kwa kebehi huku akiwa anafahamu sababu za baba kupinga vikali mipango ile ya kaka Imran kunioa mimi.

“Imran mwanangu kumbuka aibu aliyotutia yule binti, leo hii unakomaa heti ufunge naye ndoa! Hivi inaingia akilini kweli jamani?” Baba alijaribu kutafuta visingizio na sababu ya kuleta kipingamizi.

“Lakini Baba yaliyopita yameshapita hatuyakumbuki tena, mwache kaka Imran atimize ndoto yake” Mainaya alizungumza.

“Kama ni hoja ya kutimiza ndoto basi mimi namshauri amuoe Bupe!” alizunumza Baba huku amekaza sura.

“Bupe yupi mjomba?” dada Mainaya alihoji huku ametia macho na masikio ameyasimamisha kusikia jibu kutoka kwa baba.

“Bupe yule aliyekuwa na mgahawa pale nyumbani” Baba alizungumza kwa msisitizo.

“Tobba yarabi Tobba!” alihamaki kaka Imran huku ametumbua macho kwa mshangao na kusababisha mama pamoja na dada Mainaya kuangua kicheko.

Dada Mainaya alicheka hadi akapaliwa na mate. Alikohoa mara kadhaa mfururizo huku akipiga piga kifua hake kutuliza kile kifua.

“Sasa kinachowachekesha ni kipi?” Baba alihoji huku akiwa macho makavu kuashiria kuwa alikuwa anamaanisha kwa wazo alilolitoa.

“Kwanini usimuoe wewe huyo Bupe wako kama umeona anafaa!” mama alizungumza kwa msisitizo.

“Ni kweli, Bupe anahitaji sana kuolewa lakini vijana hamumuoni mnaishia kufakamia wasichana wa kazi” Baba alizungumza.

“Baba bwana hayo ndio Manini tena? Mimi nimekwambia tayari nina mhumba, huko kwa Bupe tena kutafuta nini?” kaka Imran alizungumza kwa kulalamika.

“Sikia Bro, wazee wameshabariki kitambo, haya mengine wala yasikuchanganye ni masihara tu” mainaya alizungumza kwa tabasamu akiamini maneno ya baba yalikuwa ni masihara.

“Shika adabu yako we mtoto! Nimeshasema kama ni suala la ndoa tuzungumzie ndoa baina ya Imran na Bupe full stop” alizungumza baba kwa msisitzio.

“Kwanini umemng’ang’ania huyo Bupe wako?” mama alihoji.

“Inamaan hamfahamu kinachoendelea kati ya Imran na Bupe! Au mnajichetua tu?” alizungumza Baba kwa msisitizo.

“Baba hakuna kinachoendelea kati yangu mimi na Bupe, na hata kama kingekuwepo chaguo langu mimi ni Mwantumu” alizungumza kaka Imran kwamsisitizo mkubwa.

“Wala huna sababu ya kujieleza Mwanangu, mimi nimekuunga mkono, utamuoa Mwantumu” mama alizungumza kwa msisitizo.

“Mimi nikiwa kama Baba nimesema hakuna ndoa kati yako na Mwantumu” Mzee Sekiza alizungumza kwa hasira na kuinuka kwa jazba. Alizunguusha maho yake kuwatazama wote pale mezani kisha akaachia tabasamu la ubabe na kuvuata hatua kuondoka.

“Shangazi hivi Mjomba amekuwaje?” Mwantumu akahoji kwa mshangao.

“Baba yenu ana mapepo sikuhizi na pale yamempanda, kushuka kwake hadi apepewe” mamanaye alizungumza na kuinuka kwenye kiti. Alichukua pochi yake na kuiweka begani.

“Kwahiyo mama inakuwaje?” kaka Imran alihoji kwa sauti ya mashaka.

“Jiandae kwa mchakato wa ndoa” mama alizungumza na kuondoka pasipo kuaga na kuwaacha Mwantumu na kaka Imran wametumbua macho wakiwashangaa wazazi wao. Hawakuelewa wawili wale walikuwa wamepatwa na nini. Wakaamini ni lazima nyuma ya pazia kungekuwa na kitu kilichokuwa kikiwasumbua wawili wale. Hata hivyo hawakujali sana na badala yake wakapeana pongezi kwa hatua waliyokuwa wamefikia hadi wakati huo.

******

Pamoja na kwamba nilikuwa nimefutilia mbali masuala ya mahusiano na kuyachukia kama ambavyo awali yalikuwa yamenichukia, lakini moyo ni kigugumizi kizito jamani. Kusema ukweli kabisa nilijikuta nikimpenda Fadhili.

Kama ambavyo nilimfundisha Fadhili kuwa akitaka kuuteka moyo wangu aache kuimba ule wimbo maarufu wa Nakupenda, ndio wanaume wengi wamekariri kuwa kumpata mwanamke ni kumwambia kuwa Nakupenda. Labda wanawake wengine lakini ukikutana na mwanamke wa dizaini yangu, neno Nakupenda halina ushawishi hata kidogo.

Fadhili aliendelea kunifanyia mambo mbalimbali yakiwemo ya kuonesha kunijali na kunithamini. Fadhili alikuwa mtaratibu na mwenye kunisikiliza. Mara kwa mara alitumia muda wake kunipa ushauri wa kimaisha mtego ambao wanawake wengi wanashindwa kujinasua. Fadhili alifuta kabisa dalili za kuonesha kuwa ananitaka na badala yake akawa ananitendea mema kama vile ni wajibu wake. Fadhili hakuonesha wivu kila aliponikuta katika mazingira ambayo mwanaume kama kaka Imran asingeweza kuvumilia. Nafikiri alikuwa anajua nini alikuwa anakifanya. Hakika Fadhili ndiye aliyekuwa chaguo langu kwa wakati huo.

Kama ambavyo mimi lilikuwa nimemkubali Fadhili kimwili, ndivyo nafsi na roho yangu navyo vilivyokuwa vimempokea kijana yule. Kama ambavyo hakuna mkate mgumu ndani ya chai ndivyo ambavyo hapakuwa na ugumu wa kuukabidhi moyo wangu kwa Fadhili.

Ndio narudia kusema kuwa Fadhili ndiye alikuwa mwanaume pekee ambaye angeweza kupewa fursa ya kuumiliki ule mwili uliokuwa ukiwatesa wanaume wengi wa Dar na mikoani.

Nikiwa nje ya nyumba nikifanya shughuli ya kufua nguo za mama, nilisikia sauti ya geti ikigongwa taratibu. Niliwacha kufua na kusimama kuangalia kule getini ambako kulikuwa na mtu anagonga mlango.

“Naniii?” nilipaza sauti na kuhoji lakini sikujibiwa na badala yake geti lile liliendelea kugongwa.

Nilijifuta mikono yangu kwa nguo kavu kisha nikavuta hatua kuelekea getini huku nikiwa sifahamu mtu aliyekuwa akigonga mlango ule alikuwa ni nani. Ndugu msomaji nilipofungua geti sikuweza kuamini macho yangu kwa kile nilichokuwa nakishuhudia.




Alilikuwa ni dada Bupe ametangulizana na yule kijana Shebughe niliyekutana naye ndani ya basi nilipokuwa naelekea Tanga.

“Karibuni..” niliwakaribisha huku nikiwa na hali ya mashaka juu ya ule ujio wao.

“Asante mrembo, upo na nani ndani?” alihoji dada Bupe kwa sauti ya chini.

“Nipo mwenyewe tu” nikajibu kwa sauti ya upendo.

“Kama ni hivyo tunakaribia” dada Bupe alizungumza kwa furaha huku akiingia ndani na kufuatiwa na Shebughe.

“Na huyu umemtoa wapi?” nikahoji kimasihara baada ya kumuona Shebughe na dada Bupe wakiwa pamoja.

“Kumbe mnafahamiana?” dada Bupe alijifanya kuhoji.

“Hata sikumbuki nilionana naye wapi, lakini sura yake sio ngeni” na mimi nikazungumza kwa masihara.

“Utakuwa umenifananisha mimi hata sikufahamu” Shebughe naye akajibu kwa masihara.

“Karibuni ndani” niliwakaribisha wageni wale kwa heshima.

“Hapana we lete viti tukae hapa hapa nje, ndani joto bwana” dada Bupe akazungumza kwa kujiamini huku akivuta hatua kusogea kule nilipokuwa nikifulia.

Niliingia ndani na kutoa viti huku nikiamini ugeni ule ulikuwa ni wa kaka Imran kwasababu Shebughe alikwishafika nyumbani pale pamoja na kaka Imran.

“Karibuni” nilizungumza huku nikiwapatia viti.

“Naona una kazi ya udobi mdogo wangu, pole sana” dada Bupe alizungumza.

“Ni jukumu langu dada Bupe” nikazungumza kwa bashasha.

“Sasa sikiliza Tumu mdogo wangu, mimi naona tusipoteze muda” Dada Bupe alizungumza na kumeza mate.

Niliketi kwenye kigoda na kumsikiliza kwa umakini dada yangu yule ambaye alikuwa ni rafiki yangu wa karibu sana siku za nyuma.

“Unamfahamu huyu kijana?” Bupe alizungumza kwa umakini mkubwa.

“Huyu Sheby, namfahamu vizuri sana” nikazungumza huku nikimtazama Shebughe usoni na kumzawadia tabasamu la karibu mgeni.

“Alishawahi kukueleza kuwa anakupenda?” Dada Bupe aliuliza swali ambalo liliushitua kidogo moyo wangu na kusababisha mapigo ya moyo kuongezeka spidi kwa kiasi fulani. Nikajikuta nikipata kigugumizi kutoa jibu la swali lakekwasababu sikuwa nimelitegemea.

“Nijibu basi Tumu wangu” dada Bupe alizungumza kwa kubembeleza.

“Hapana, sikumbuki vizuri” nikajibu kwa kujilazimisha.

“Sasa huyu ni mdogo wangu kabisa” dada Bupe alizungumza kwa msisitizo.

“Yani huyu Shebughe ni ndugu yako?” nikahoji kwa mshangao.

“Damu moja, yani toka nitoke” dada Bupe akakazia maneno yake.

“Inawezekanaje Msambaa wa Magoroto akawa na undugu wa damu na Mnyakyusa wa Tukuyu?” nikahoji kwa mshangao mkubwa kwasababu kila mmoja nilikuwa nikimfahamu vizuri sana.

Swali langu lile lilionekana kumchanganya kidogo dada Bupe na kukosa jibu la kunipa na badala yake akawa anajikuna kichwani. Aliamini sasa njia ya muongo ilikuwa imenaswa na pengine malengo yao yangegonga mwamba.

“Mama yetu ni mmoja isipokuwa baba zetu ndio tofauti” Shebughe alidakia na kutoa jibu ambalo hata dada Bupe hakuwa amelitegemea.

“Kwahiyo wewe ni kaka yangu, maana huyu ni dada yangu?” nikazungumza kwa msisitizo.

“Sasa hilo ndilo lengo kubwa lililotuleta hapa, tunataka wewe uwe zaidi ya rafiki” alizungumza dada Bupe kwa msisitizo huku akinikodolea macho.

“Hata hivyo sisi ni zaidi ya rafiki” nikasema.

“Hapana sio kihivyo Tumu”

“Kumbe?”

“Naomba ukubali kuolewa na kaka yangu” alizungumza dada Bupe kwa sauti ya kubembeleza.

Niliposikia maneno yale kutoka kwa dada Bupe sikuweza kuamini masikio yangu. Nilifikiri tabia ile ya kukuwadia watoto wa wenzake alikuwa ameiacha kutokana na matatizo yaliyomkuta kumbe bado alikuwa vilevile. Ama kweli tabia ni ngozi unaweza kuibadilisha rangi ikaonekana tofauti lakini itaendelea kuwa ni ileile.

Niliinua macho yangu na kumtazama dada Bupe usoni kisha nikameza funda la mate na kuuma meno yangu kwa nguvu.

“Hapana dada Bupe sipo tayari” nikajibu kwa ufupi.

“Mdogo wangu Sheby sio kama wale washenzi wa kipindi kile” alisema dada Bupe kwa kubembeleza.

“Dada Bupe mbona mimi tayari nina mchumba, na ninampenda sana” nikazungumza kwa sauti ya upole lakini iliyokuwa imejaa msisitizo.

“Achana na wakina Imran mdogo wangu watakupotezea muda bure” Bupe alizungumza.

“Hapana dada Bupe ninampenda sana mchumba wangu” nikazungumza kwa msisitizo zaidi.

“Sasa sikiliza Tumu mdogo wangu, mpe nafasi Sheby halafu utapima mwenyewe ni nani kati yao anayekupenda kwa dhati” Bupe alizungumza maneno ambayo yalizidi kunifanya nimshushe thamani na kumuona mshenzi.

“Hivi unafahamu kama Tumu wa leo sio Yule wa kipindi kile?” nikahoji kwa msisitizo huku nikionekana wazi kuwa sikuwa nimependezwa na mazungumzo yale.

“Wewe ni Mwantumu yule yule mdogo wangu!” dada Bupe akazungumza kwa msisitizo.

“Wacha kujidanganya dada Bupe!”

“Wewe ni yuleyule, tofauti ni kwamba Mwantumu wa leo amekuwa mkubwa na anajitambua tofauti kabisa na Mwantumu yule wa zamani” dada Bupe alizungumza kwa nia ya kunipamba na kutafuta urahisi wa kufanikisha malengo yake.

“Vizuri dada Bupe. Sasa ni hivi kwa sasa sihitaji mwanaume na wala sitaki kuolewa” nikazungumza kwa msisitizo.

“Mbona kama vile ni ugomvi mdogo wangu?” Bupe akahoji kwa mshangao baada ya kuniona nimebadilika ghafla.

“Nafanya hivi ili usinizoee” nikasisitiza.

“Ndwadwa, kama kupenda ni kosa basi wacha ninyongwe” Shebughe akaingilia kati baada ya kuona msimamo wangu.

“We koma, mimi siitwi Ndwadwa!” nikajikuta nikizungumza kwa jazba huku nikitetemeka kwa hasira. Sikuopenda kabisa ile tabia ya dada Bupe kunifanya kamalaya kake ka kutongozea wanaume. Dharau kubwa sana!

“Hivi na kiburi chako hicho unafahamu kama Imran ni mwanaume wangu?” dada Bupe akazungumza kwa hasira na yeye baada ya kuniona mtoto wa kitanga nimecharuka.

“Hayanihusu!” niakajibu kwa ufupi huku nikigeukia beseni la nguo kwaajili ya kuendelea na shughuli yangu.

“Sasa sikiliza binti, ninampenda sana Imran wangu!” Bupe alizungumza huku akiinuka kutoka kwenye kiti na kushika kiuno kwa nyodo.

“Kwahiyo?” nikahoji huku akisungua nguo.

“Nitahakikisha nakusambaratisha kabla hata ya hiyo ndoa yenu” Bupe akazungumza kwa hasira huku akinielekezea kidole cha onyo.

“Heheeee Halo ya kuku Kwiyo kunguru yake Kwao!” Nikajichekesha kwa sauti ili kumuudhi mwanamke yule.

“We niletee ushankupe wa kitanga! Nitaichafua hiyo sura yako hadi Imran asikutamani tena” dada Bupe alizungumza kwa kebehi na kusahau kabisa kama yeye mwenyewe alikuwa ameshachafuliwa sura yake na kuonekana kama kinyago.

“Basi dada Bupe nyamaza utaharibu kabisa” Shebughe alizungumza huku akijaribu kumshika mkono dada Bupe kumtoa ndani mle.

“Kaone kwanza kasura kabayaa utafikiri kinyago! Ungekuwa mzuri we dogo sijui kama tungekunywa maji” jamani nyie mwanamke yule alizidi kuzungumza kwa kunibeza.

“Heri yako wewe mwenye sura. Sisi vinyago wenye sura za vibandiko tuacheni!” nikajikuta na mimi nikizidi kutokwa na maneno machachu kwani ipi bwana, Eboo!

“Unakaona Sheby! Unakaona haka katoto kamekuja juzi tu nimekafundisha mwenyewe hata kuvaa leo hii kananitusi mimi!” dada Bupe akajikuta akizidi kupandwa na hasira. Hakutegemea kabisa kama angekuja na kukutana na Mwantumu wa aina ile. Alivuta hatua kwa hasira kutaka kunivaa na kunitandika makofi.



“Weweee! Cheza mabli na chombo hicho!” ilikuwa ni sauti ya kaka Imrani aliyekuwa akiingia kupitia geti dogo.

Kumbe muda wote ule tuliokuwa tukibisha na dada Bupe, kaka Imran alikuwa amejibanza kwenye geti akisikiliza mazungumzo yetu yale.

Dada Bupe na Shebughe wakajikuta katika mshangao mkubwa baada ya kumuona kaka Imran akivuta hatua kwa mwendo wa pole pole kuelekea pale tulipokuwa tunazungumza. Alipofika alipeleka macho yake na kumtazana Shebughe kwa dharau na kuachia tabasamu la kebehi.

“We umeishi Tanga kwenye chemchem ya warembo, umeshawahi kuona chombo kama hiki tangu uzaliwe?” alihoji kaka Imran kwa sauti ndogo ya kebehi.

“Huyu Malaya ndiye anayekufanya umevunja makubaliano yetu” dada Bupe alizungumza kwa hasira.

“Malaya ni wewe uliyeungua sura kwa kazi ya kusaka wanaume. Naomba uondoke haraka” kaka Imran aliendelea kuzungumza kwa sauti ya taratibu pamoja na kwamba maneno yake yalikuwa yanawasha.

“Mungu anakuona Imran, uliniahidi mambo mengi leo hii umemuona huyu shetani ndio unaniona mimi wa nini?” dada Bupe akazungumza kwa kulalamika.

“Aisee we Shebughe hebu kusanya hizi takataka zako na uondoke nazo hakuna dampo hapa” kaka Imran akazungumza kwa msisitizo ingawa ilikuwa ni sauti ya upole.

“Sasa sikiliza we mwanaume, unataka utanioa hutaki utanioa” dada Bupe alizungumza kwa msisitizo.

“Ni lazima akuoe atake asitake!” ilikuwa ni sauti ya Mzee Sekiza ambaye naye alikuwa akiingia getini.

Watu wote tuligeuza shingo zetu na kuangalia getini ambako Baba alikuwa akitembea kwa hatua ndefu kuingia ndani.

“Baba hawa watu wanaleta vurugu humu ndani” kaka Imran akazungumza kwa hasira.

“Ni mara ngapi nilikuwa nikikuonya kuwana mahusiano na Bupe lakini uligoma na kuniambia kuwa unataka kufunga naye ndoa?” Baba alihoji kwa umakini mkubwa.

“Ya kale hayanuki baba, mimi siwezi kufunga ndoa na kituko hiki” alizungumza kaka Imran kwa msisitizo.

“Kwasababu amepata ajali ndio unamuita kituko?” Baba alizungumza.

“Mimi na yeye tulishaachana kabla hata hajapata hiyo ajali” kaka Imran akazungumza kwa msisitizo.

“Haijalishi, nimesema utamuoa Bupe utake usitake!” alizungumza Baba na kuvuta hatua kuingia ndani.

Dada Bupe alimtazama kaka Imran kwa macho ya kebehi huku akichezesha chezesha midomo yake kiushindi.

“Kama hutaki radhi za baba yako, pingana na maneno yake” Bupe alizungumza huku akichukua pochi yake kutoka kwenye kiti na kuiweka begani.

Shebughe hakuingilia mazungumzo yale kwasababu yalikuwa yakimgusa moja kwa moja. Aliamini kabisa kama kaka Imran angemuoa dada Bupe basi mimi ningekuwa wa kwake. Hivyo aliomba Mungu sana baba mzee Sekiza kuongeza msisitizo katika kuhakikisha kaka Imran anafunga ndoa na dada Bupe.

“Lakini kaka mkubwa ungesikiliza maneno ya mzee” Shebughe alijaribu kushawishi na kuongeza uzito wamaneno ya Baba.

“Nyamaza na wewe mnafki mkubwa! Unajifanya ni rafiki kumbe unataka kunipindua!” kaka Imran akazungumza kwa hasira zaidi baada ya kusikia ushauri ule wa Shebughe.

“Twende zetu Sheby. Labda kama mimi sio mtoto wa kinyakyusa! Nitahakikisha malengo yangu yanatimia” dada Bupe alizungumza huku akivuta hatua kuelekea getini na Shebughe akimfuata nyuma kama mbwa na mkia wake.

“Pelekeni Korona zenu huko!” Akasema Imran kwa kebehi.

“Kwanza hata hawajaosha makono yao” nikakazia.

“Mnataka kumuua Tumu wangu kwa Korona sio?” akasema Imran.

“Imran angalia mdomo wako huo!” Shebughe akazungumza kwa hisia kali.

“Kelele we sigara nyota! Nikikukuta tena hapa nakukata miguu yako hiyo!” kaka Imran alizungumza kwa hasira.

“Wacha vitisho vyako wewe, tunaondoka na tutarudi hata mara kumi” dada Bupe akazungumza kwa msisitizo huku wakitoka ndani mle.

Kaka Imran akatikisa kichwa kusikitika na kuingia ndani akiniacha mimi nikiwa hoi bin taaban pale nje kutokana na mzigo wa mauzauza uliokuwa umeletwa na Dada Bupe na Shebughe wake.

*****

Usiku pekee ambao hautatokea kusahaulika katika maisha yangu, ni usiku ambao moyo wangu ilishirikiana na Nafsi yangu kuushawisi mwili wangu. Ni usiku ambayo nilikuwa nimeamua kufahamu ukweli na hatma ya maisha yangu kimahusiano.

Visa na vituko kutoka kwa wanaume vilikuwa vikiongezeka kila kukicha na kuniweka katika wakati mgumu. Lakini usiku huo niliuona kama vile ulikuwa usiku wa ukombozi kwa upande wangu.

Nakumbuka usiku huo nilikuwa nimejilaza kitandani huku mawazo yangu yakiwa juu ya kijana Fadhili. Ni usiku ambo nilikuwa nikiomba muujiza utokee na kijana Fadhili aingie chumbani kwangu na kunikumbatia huku akinimiminia mvua ya mabusu. Nilitamani sana kumtazama Fadhili usoni pasipo kupepesa macho ili kuona namna macho yake ambavyo yangezungumza na macho yangu. Hata hivyo Fadhili hakutokea na wala hapakuwa na dalili yoyote ile ya ugeni usiku huo.

Nilijikuta uvumilivu ukinishinda mtoto wa kike na kujiinua kutoka pale kitandani. Niliketi kitako kwa sekunde kadhaa kisha pasipo kujadili wala kufikiri nikajiinua na kutoka chumbani kwangu. Moja kwa moja nikaenda kusimama kwenye mlango wa chumba cha Fadhili.

Kwa tahadhari kubwa sana niligonga mlango wa Fadhili huku nikigeuka kulia na kushoto kuona kama kungetokea mtu na kunikuta nimesimama pale mlangoni. Mungu si Athumani, Fadhili alifungua mlango na kuchungulia nje huku akionekana usingizi ungali umemtawala.

Fadhili alipotazama vizuri na kuniona mtoto wa kike nikiwa nimesimama mlangoni kwake huku nimevalia night dress, ile nguo laini ya kulalia akashituka kidogo na kuhisi usingizi wote ukitoweka.

Kabla hata hajazungumza neno lolote mtoto wakike nikamsukumia ndani na mimi nikaingia na kwenda kujitupa kitandani. Fadhili akawa kama vile amepagawa akinikodolea macho ya mshangao pale kitandani ambako nilikuwa nimejilaza chali nikimtazama huku mguu mmoja nikiwa nimeukunja na kupelekea sehemu kubwa ya mapaja wangu kuwa wazi.

“Upo sawa wewe?” Fadhili akahoji kwa mshangao.

“Funga mlango” nikazungumza kwa sauti ya kukatakata.

Nikamuona Fadhili akijikanyaga kanyaga kwasababu hakuwahi kuniona nikiwa katika hali kama ile. Pamoja na kwamba alikuwa akinipenda sana lakini kitendo changu kile kilimpumbaza na kuwa kama vile mlevi wa komoni.

Nilipoona kijana yule amezubaa nilijiinua kutoka pale kitandani na kumfuata kwa spidi na kumkumbatia kisha nikampiga busu moja matata ambalo nafikiri lilizidi kumchanganya.

“Naomba usinipotezee muda Fadhili kuna mambo nahitaji kufahamu” nikazungumza kwa msisitizo huku nikiwa nimemkumbatia na kumkazia macho kwa msisitizo.

“Unataka kufahamu nini Tumu?” alizungumza Fadhili huku mapigo ya moyo wake yakienda mbio baada ya chuchu zangu zilizokuwa zimesimama kama sindano zikigusa kifua chake ambacho kwa wakati huo hakikuwa na nguo.




“Nataka kujua kama kweli unanipenda” nikazungumza kwa sauti ya chini lakini iliyojaa ubabe wa mahaba.

“Inamaana hadi muda huu haujafahamu jambo hilo?” Fadhili alihoji kwa sauti nzito kidogo tofauti na sauti yake ya siku zote.

“Hebu niambie kama unanipenda” nikahoji.

“Nikwambie nini sasa?” Fadhili akahoji

“Nambie unanipenda!” nikasisitiza.

“Hayo mashairi ulinikataza nisiyaimbe, na mimi siwezi kuyaimba tena” Fahili alizungumza kwa sauti ya upole.

“Kwahiyo hunipendi?” nikahoji kwa kulalamika.

“Ni kwanini unasema sikupendi?”

“Kwasababu hutaki kuniambia kuwa unanipenda” nikazidi kulalamika.

“Haya Nakupenda Tumu wangu” Fadhili alizungumza na kunikumbatia huku akinipiga busu la kwenye paji la uso.

Lile neno Nakupenda niliweza kuliona uzito wake siku hiyo. Niliamini kuwa Fadhili alilitoa neno lile kutoka ndani ya nafsi yake babisa huku akiwa anamaanisha ananipenda kweli.

“Ni nini hatma ya kunipenda kwako?” nikazungumza kwa msisitizo.

“Mbona leo umekuwa mbabe hivyo?” Fadhili akahoji baada ya kuniona nikizungumza kwa sauti ya kijeshi.

“Nataka majibu na sio maswali” nikasema.

“Nataka uwe mama wa watoto wangu, nami niwe baba wa watoto wako” Fadhili alizungumza kwa sauti ya kubembeleza huku akichezea nywele zangu na kuzidi kunichanganya.

Maneno ya Fadhili yalinifanya nihisi kama vile nilikuwa nimepandwa na pepo. Nafikiri ni kweli nilikuwa nimepandwa na pepo la ngono kwasababu nilimvuta kwa nguvu Fadhili na kumdondoshea kitandani. Kabla hata hajashangazwa na kitendo kile tayari mtoto wa kike nilishafika juu yake na kumkalia kiunoni huku mguu mmoja nimepiga goti.

Ndugu msomaji kumbe nilikuwa najaribu kuuwasha moto pasipo kujitambua. Fadhili alijiinua na kunirusha kidogo juu kisha akanidaka na kunilaza kitandani na yeye akawa amenilali kwa juu huku akinitazama machoni.

Niliachia tabasamu la mahaba na kufumba macho kidogo huku shingo nikiigeuzia pembeni kukwepesha kutazamana naye machoni. Kitendo bila ya kuchelewa midomo ya Fadhili ilinasa kweye madafu yangu ya kifuani na kuanza kucheza nayo. Sijui nizungumze nini kwa ile hali ambayo nilikuwa nikijisikia kwa kitendo kile alichokuwa anakifanya kijana yule.

Nikiwa nimedata kwa kitendo kile, mkono wake wa kuume ulizunguuka na kutarai taratibu kwenye madafu ya uani. Ukono ule ulitembea bila breki hadi usawa wa mapaja yangu na kuweka kambi ya dakika chache kabla ya kuhamia nyuma ya magoti.

“Oooh..Fa..fa…Da..ni…Dhili!” nikajikuta nikizungumza maneno yasiyoeleweka.

Sikuweza kujibu mashambulizi kwa namna yoyote ile nafikiri ni kutokana na kuzidiwa. Hata hivyo uvivu wangu Fadhili haukumkera kwani alihamishia midomo yake na kwa kutumia ndimi alisafisha pingili za shingo yangu na kunifanya nitote chapaa kwa jasho.

“Fadhili leo nimekupa…chukua Fadhili chuku…chuku..chukuaaaah!” nikaendelea kulalamika kitoto cha watu.

Sauti yangu nafikiri ilichangia kumuongezea utundu Fadhili kwani ulimi ulihamia masikioni. Hapo sasa nilipoteza kabisa muelekeona sikuelewa tena kilichokuwa kimeendelea kwasababu kila sekunde kijana Fadhili aliongeza madoido na kunichanganya zaidi.

Baada ya dakika kadhaa mtoto wa kike nikajikuta hoi bin taaban huku nimejilaza chali guu moja mashariki na lingine magharibi.

“Tumu..” niligutushwa na sauti ya Fadhili kutoka katika usingizi mzito uliosababishwa na uchovu. Nilifumbua macho na kumkuta Fadhili ameniinamia huku akitabasamu. Nikampokea kwa tabasabu kisha nikafumba macho kwa viganja vya mikono kutokana na aibu.

“Vipi unauonaje ulimwengu wa mapenzi?” Fadhili alihoji kwa sauti yake ndogo lakini iliyokuwa nzito.

“Umenipora usichana wangu, ole wako usinioe” nilizungumza huku nikiinua mkono na kumshika kidevu.

“Utanifanya nini?”

“Nitakutoa roho!, kweli vile nitahakikisha nakuua kwa mikono yangu mwenyewe” nilizungumza kwa ile sauti yangu ya mahaba lakini nilikuwa namaanisha kwa kile nilichokuwa nimekisema.

“Siwezi kukuacha Mwantumu, sikutegemea kabisa kama mambo yangekuwa kama hivi yalivyo” Fadhili alizungumza kwa msisitizo.

“We zungumza tu”

“Hongera sana, ni wasichana wahache sana wenye umri kama wako wakawa sild” Fadhili alizungumza huku akichezea pua yangu.

“Wacha pua yangu huko!” nilizungumza kwa kudema huku nikichukua mkono wake na kuukumbatia kifuani.

“Nikupe tena kidogo basi” Fadhili alizungumza huku akipeleka mkono wake na kupapasa dafu langu la kushoto.

“Hapana Fadhili kwa leo inatosha kabisa, tufanye siku nyingine” nilizungumza huku nikimshika mkono wake na kuuweka pembeni kisha nikajiinua kutoka pale kitandani.

“Unakwenda wapi sasa?” Fadhili akahoji.

“Nakwenda kulala” nikazungumza kwa kudeka.

“Tulale wote leo mpenzi wangu” alizungumza Fadhili huku akiweka viganja vyake kwenye mashavu yangu.

“Umeniitaje?” nikahoji kwa furaha baada ya kusikia Fadhili ameniita mpenzi wake.

“Mpenzi wangu!” Fadhili alizungumza kwa msisitizo huku akinifinya kwenye mashavu.

“Basi mie nakwenda zangu”

“Unakwenda wapi?”

“Nimekwambia chumbani kwangu kulala! We kaka huelewi kiswahili” nilizungumza kwa kudeka huku anikijivalisha ile nguo yangu ya kulalia ambayo sikufahamu ni nani aliyekuwa amenivua na muda gani.

Fadhili alitulia kitandani akinitazama kwa macho ya huba huku akiachia tabasamu mwanana la mahaba na ushindi. Hakutegemea kabisa katika maisha yake kama ingetokea angalau siku moja akaonja utamu kutoka kwa mtoto wa kitanga.

“Nini?” nilihiji baada ya kumuona akinitazama kwa yale macho yake ya kumchuzi.

“Hakika umebarikiwa kuliko wanawake wote” alizungumza Fadhili huku akinitazama maeneo ya kati.

“Unanichungulia enh?”

“Akuuu!” Fadhili akajibu kimahaba kama ambavyo nilikuwa nimezungumza mimi.

Nilivuta hatua na kumpiga busu kisha kabla hata hajashangazwa na kitendo kile nilishafika mlangoni na kufungua mlango tayari kwa kuondoka.

“Kwaheri baba watoto” niligeuka na kumuaga kwa sautiya kudeka kisha nikachomoka chumbani mle na kumuacha ameduwaa akinikodolea macho kama vile hakuwa anaamini kwa ambacho kimetokea usiku huo.

Baada ya kutoka chumbani mwa Fadhili huku nikiwa na furaha ndani ya nafsi yangu, niliufunga malango ule taratiibu na kugeuka kwaajili ya kuondoka kurudi chumbani kwangu.

Laahaula! Kumbe dada Mainaya alikuwa amesimama mlangoni kwake akinikodolea macho jinsi nilivyokuwa nikifunga mlango wa chumbani kwa Fadhili na kuanza kutembea kwa kunyata kama mwizi.

“Haya habari za huko mama!” sauti ya dada Mainaya ikanigutusha na kunifanya nigeuke nyuma kumtazama.

“Huko utokako hawajambo?” Mainaya akahoji tena kwa kebehi.




“Shikamoo dada!” nikajikuta nikisalimia bila kujipanga.

“Hivi wewe mwanamke mbona mchafu hivyo? Wanaume wote humu ndani umeshavuruga. Nilidhani Fadhili amepona kumbe naye umeshamaliza! Huoni aibu wewe” dada Mainaya alizungumza kwa kulaumu.

“Lakini dada Naya mbona sikufanya kitu chochote kibaya” nikajifanya kuzungumza kwa kulalamika kama vile alikuwa ananionea.

“Haya pamoja na ufirauni wako lakini bado Imran anataka kufunga ndoa na wewe, haitoshi unachukua na mdogo wake kweli jamani?” Dada Mainaya akazungumza maneno ambayo hayakuniingia akilini. Yaani yeye bado alikuwa na mpango wa mimi kuolewa na Imran.

“Naomba unisamehe dada Naya, lakini kusema kweli nampenda sana Fadhili” nikaamua kuweka wazi hisia zangu kwa Mainaya.

“Nyoo laana wewe, unampendaje Fadhili ilhali unafahamu kuwa wewe ni mchumba wa Imran” alizungumza kwa kujiamini Mainaya.

“Lakini dada Naya ni kwanini unanilazimisha niolewe na Imran wakati unafahamu kuwa mimi ninampenda Fadhili?” nikazungumza kwa msisitizo lakini kwa sauti ya chini.

“Hebu potea mbele ya macho yangu, nisije nikatapika!” alizungumza dada Mainaya kwa hasira.

Pasipo kuongeza neno lolote lile niligeuka na kuelekea chumbani kwangu kujipumzisha, ukizingatia zaidi nilikuwa nimejawa na uchovu kutokana nashughuli niliyokuwa nimetoka kushughulika.

******

Pamoja na kwamba ndani ya nafsi yangu kulikuwa kumejawa na furaha kutokana na kufanikiwa kulinasa na kuliteka penzi la Fadhili lakini bado kulikuwa na vitu ambavyo viliniandama kwa lengo la kutenganisha nafsi zetu mimi naFadhili.

Siku hiyo nilishangaazwa sana na kitendo cha watu wote kuto kwenda kazini. Sikuwa nafahamu ni jambo gani ambalo liliwafanya watu wale wote kubaki nyumbani siku hiyo.

“Babeee” nikagutushwa na sauti ya Fadhili ikiniita kwa mbwembwe na mapozi nilipokuwa kwenye karo nikisafisha vyombo.

Nilipogeuka na kumuona Fadhili nilihisi mapigo ya moyo wangu yakienda mbio. Sijui ni kitu gani kilikuwa kimenikumba mwenzenu mimi kwa kijana yule. Nikaachia tabasamu huku nikikwepesha macho yangu kwa aibu.

“Vipi mrembo wangu nikusaidie?” Fadhili alizungumza kwa sauti ndogo huku akisogea hadi pale nilipokuwa nimesimama na kunishika kiuno.

“Unaweza kuosha vyombo wewe?” nikahoji kwa sauti ya kubana kimahaba.

“Hata wewe ukitaka naweza kukuosha” Fadhili akazungumza huku akinipapasa maeneo ya kiunoni na kupelekea hisia kali zilizopanda hadi kwenye moyo.

“Najua maana jana usiku uliniosha kisawa sawa!” nikazungumza kwa utani huku nikisuuza sahani.

“Nichumu basi kidogo!” Fadhili akazungumza kwa sauti nzito.

“Kwanza toa huo mkono wako usije ukanipandisha nanihii bure!” nikazungumza huku nikitabasamu na macho nikiyarembua utadhani mwali aliyelishwa kungu.

“Zikipanda si tunazishusha tu” Fadhili akajibu kwa ile sauti yake nzito.

“Kwanza kwanini leo hamkwenda kazini?” nikabadilisha mada baada ya kuona kijana yule alikuwa akielekea kubaya.

“Ah wanasema kuna kikao cha familia” Fadhili akajibu.

“Mbona mimi sikuambiwa au mimi sio mwanafamilia?” nikahoji pasipo kumtazama Fadhili usoni.

“Hata mimi mwenyewe sikuambiwa ajenda za kikao” Fadhili alijibu kwa ufupi.

Maneno ya Fadhili yalinishitua kidogo nikahisi kikao kile kilikuwa kikihusu kunijadili mimi bada ya dada Mainaya kunifuma nikitokea chumbani mwa Fadhili jana usiku.

“Ni nani aliyeitisha hiki kikao?” nikahoji kwa umakini mkubwa.

“Bi mkubwa”

“Au kuna tatizo?” nikahoji kwa mashaka.

“Mbona una wasiwasi?” alihoji Fadhili baada ya kubaini kuwa nilikuwa na mashaka na kile kikao.

“Unajua jana dada Mainaya aliniona nilipokuwa nikitoka chumbani kwako” nikazungumza kwa msisitizo mkubwa.

“Wacha utani Tumu!” Fadhili akashituka baada ya kupokea taarifa ile.

“Vipi unaogopa?”nikahoji

“Hapana, sikuwa nimetegemea jambo kama hilo” Fadhili alijibu.

“Basi tegemea lolote kwa hilo” nikazungumza huku kwa upande wangu nikiwa tayari kwa lolote lile ambalo lingetokea kutokana na kile kitendo cha Dada Mainaya kunikamata nikitokea chumbani kwa Fadhili.

“Nakupenda sana Mwantumu, nitakuwa tayari kwa lolote lile hata kama kukuoa kesho” Fadhili alizungumza huku akizunguusha mkono wake kwenye mabega yangu na kunikumbatia.

“Malizieni kabisa maana haitakaa ijirudie tema milele daima” sauti ya dada Mainaya ilitugutusha kutoka kwenye maongezi yetu.

“Ooh Sister huyo!” Fadhili alishituka na kumsemesha dada Mainaya.

“Mnaitwa ndani kikao kinataka kuanza” Mainaya alizungumza kwa sauti ya msisitizo.

“Tunaitwa wangapi?” Fadhili akahoji.

“Nyote, mnasubiriwa ninyi tu” alizungumza dada Mainaya na kuelekea sebleni.

Fadhili akanikonyeza na kunipa ishara ya kuongozana naye kuelekea kwenye hicho kikao cha familia.

Hakika kikao kile kilionekana kuwa kizito kuliko kawaida. Kila mmoja alionekana kusubiria kikao kile kwa hamasa kubwa. Watu wote walikuwepo kasoro baba Mzee Sekiza ndiye sikuweza kumuona katika kikao kile.

“Jamani jambo kubwa na la msingi katika kikao chetu hiki linamhusu Imran” Mama alifungua kikao kile kwa sentensi hiyo na kunipa ahuweni ndani ya nafsi yangu na kujikuta wasiwasi ukiniisha.

“Kaka yenu Imran anataka kuoa” mama alizungumza kwa sauti ndogo iliyokuwa imejaa upendo.

“Duh hongera sana kaka mkubwa. Kama sikosei atakuwa ni yule mtanga wako uliyetudokezea” Fadhili akazungumza kwa furaha kubwa.

“Kumbe tayari alishakudokeza enh?” mama akahoji kwa msisitizo.

“Ah kaka mkubwa alishaeleza kilakitu” alieleza Fadhili na kujifanya anaelewa mpango mzima kumbe hakuna alichokuwa anakifahamu.

Mama aliposikia maneno yale kutoka kwa Fadhili akaamini kulikuwepo na makubaliano kati ya Fadhili na kaka Imran juu ya kuwa na mimi.

“Sasa tumeshazungumza na wazazi wa binti wameridhia” mama alizungumza.

“Woow! Very nice” Fadhili akajibu kwa hamasa kubwa akiamini kitendo cha kaka kuoa ingekuwa furaha kwa upande wake kwasababu pasingetokea pingamizi katika mpango wake wa kunioa mimi.

“Tatizo ni kwamba hatujamueleza binti mwenyewe juu ya mchakato mzima” mama alizungumza.

“Aah unafeli wapi kaka mkubwa?” Fadhili akahoji kwa lawama huku akiamini kaka yake alikuwa ni mzembe katika mambo muhimu kama yale.

“Hata hivyo sio tatizo kwasababu binti mwenyewe anampenda kaka yetu” Mainaya akaingilia kati na kumtoa hofu Fadhili.

“Hapo sawa, endelea Bi. Mkubwa kutupatia uhondo” alizungumza Fadhili kwa hamasa kubwa iliyokuwa imechanganyikana na furaha.


“Na huyo binti mwenyewe ambaye amependwa na kaka yenu sio mwengine bali ni MWANTUMU” mama alizungumza kwa msisitizo huku akimtazama Fadhili kwa jicho la kumtathmini.

Maneno yale yalitushitua sana mimi na Fadhili. Kila mmoja alikuwa kama vile amemwagiwa maji ya barafu kipindi cha mvua nyingi za masika. Fadhili alishindwa kuvumilia na kuinuka kutaka kuondoka.

“We Fadhili, unataka kwenda wapi?” mama akahoji kwa msisitizo.

“Unajua sielewi mama” Fadhili akazungumza huku akionekana kuchanganyikiwa.

“Hebu keti tumalizie mazungumzo” mama alizungumza kwa amri.

“Mama ni kitu gani ambacho wewe hukifahamua?” Fadhili akahoji kwa kulaumu.

“Mwanangu wakati mwingine unatakiwa kukubali mabadiliko kutokana na nyakati” Bi Fatma akaeleza kwa sauti ya upole na kujihami.

“Kwani kuna kitu gani kinachoendelea Shangazi?” Mainaya akahoji huku akijifanya hakuwa anaelewa jambo lolote lililokuwa likiendelea kati yangu mimi na Fadhili.

“Msijali kila kitu kitakaa sawa” mama akazungumza kwasauti ya kujiamini.

Kaka Imran alikuwa ametulia kama vile hakuwepo kwenye kikao kile akimtumbulia macho Fadhili. Alikuwa amefahamu kila kitu lakini akajifanya haelewi kilichokuwa kikiendelea kwa wakati ule.

Kwa upande wangu nako mambo yalikuwa hayaeleweki. Nilikuwa kama vile nimekumbwa na jinni Bumbuwazi ambaye alinifanya nisielewe kilichokuwa kikiendelea katika kikao kile.

“Fadhili mwanangu, kuna jambo moja baya sana linaweza kutokea kama ndoa hii isipokuwepo” mama alijaribu kumueleza Fadhili kwa kituo.

“Lakini mama mjue mnatuchanganya hatuwaelewi kinachoendelea hapa!” kaka Imran akaingilia kati na kuhoji kwa msisitizo.

“Haya mambo yanachanganya wanangu!” Mama akazungumza kwa sauti ya kukata tamaa.

“Wewe ndio unatuchanganya mama, hebu weka wazi” alizungumza kaka Imran kwa msisitizo.

“Sikiliza kaka mkubwa” Fadhili akazungumza na kutufanya watu wote kwenye kikao kile kumsikiliza.

“Ngoja kwanza” Dada Mainaya akaingilia kati na kumfanya Fadhili kunyamaza na kumsikiliza yeye.

“Hapa tumekuja kujadili mambo ya msingi, hizo habari nyingine hazina nafasi muda huu” Mainaya akazungumza kwa msisitizo huku akiamini Fadhili alikuwa anataka kuchafua hali ya hewa.

“Imran hawezi kumuoa Mwantumu!” Fadhili akazungumza kwa msisitizo.

“Umekuwa Mungu tayari” kaka Imrana akazungumza kwa jazba.

“Hakuna cha Mungu wala mzungu hapa, nimesema ndoa haipo!” Fadhili akasisitiza zaidi na kuzidi kuchafua hali ya hewa.

“K e l e l e !” Bi. Fatma akapaza sauti na kuzungumza kwa ukali.

“Lakini mama mbona mnanifanyia ukatili kiasi hiki?” Fadhili akazungumza kwa kulalamika.

“Mimi ni mtu mzima Fadhili, nimeshaona mengi sana. Huwezi kujua ni balaa gani nimelizuia mbele yako” mama akazungumza.

“Mama hizo nihadithi za sungura na fisi. Mimi nilishakueleza kila kitu siku nyingi” Fadhili akazungumza kwa kulalamika.

“Ndiomaana nikakwambia uwe mpole, kwasababu kama ni hoja hiyo, kaka yako Imran alinieleza muda mrefu kuwa anataka kumuoa Mwantumu” Mama alieleza.

“Lakini mama…” Fadhili alitaka kuzungumza kitu.

“Hakuna cha lakini Fadhili mwanangu, kaka yako alishakwenda Tanga na kuzungumza na wazazi wa Mwantumu juu ya jambo hili” mama akasisitiza. Aliamua kuhakikisha kaka Imran anafunga ndoa haraka sana na mimi ili kuweza kuzuia mpango wa Baba wa kutaka kunifanya mke wa pili.

“Lakini mbona mimi mwenyewe hamnishirikishi naona mnajadiliana tu wenyewe” Ikabidi niingilie kati na kuzungumza kwa msisitizo kwasababu mwanamke aliyekuwa akijadiliwa katika kikao kile alikuwa ni mimi.

“Usijali mrembo, tumeshazungumza na wazazi wako kilakitu kipo sawa” dada Mainaya akajibu haraka akiamini kama ningeshirikishwa katika jambo lile, ningeweza kuleta kipingamizi.

“Kwani wanaolewa wazazi wangu au mimi?” nikahoji kwa mshangao mkubwa.

“Usiogope Mwantumu, kama ambavyo nilikwambia kuwa nakupenda. Nimefuata hatua zote na hadi sasa nimefikia hapa” kaka Imran alizungumza kwa sauti ya msisitizo. Akili yake haikuwa sawa kwasababu hakuweza kuelewa ni kwanini kila alipokuwa akijaribu kuzungumzia jambo lile vinatokea vipingamizi.

“Lakini mimi sipo tayari kuolewa na wewe kaka Imran” nikajibu kwa sauti ya upole lakini iliyojaa msisitizo.

“Wazazi wako wamekubali nikuoe Mwantumu” kaka Imran akazungumza kwa msisitizo.

“Hapana Imran, nenda taratibu” alizungumza Mainaya kwa tahadhari kubwa.

“Kama ingewezekana ungekaa kimya kabisa!” Mama akaongezea maneno ya dada Mainaya.

“Nikae kimya wakati hali imeshaingia ndorobo mama!” Imran kazungumza kwa jazaba.

“Hizi ndoa za kulazimishana nilizisomaga zamani kwenye kitabu cha Kibena, kumbe bado zinaishi” Fadhili alizungumza kama vile hakushirikishwa katika kikao kile.

“Sikia dogo, mimi nafahamu sana kuwa unamtamani Mwantumu. Tatizo ni kwamba tayari ameshakuwa shemeji yako. Hivyo inakupasa umuheshimu na kukaa naye mbali kabisa” alizungumza kaka Imran kwa msisitizo huku akimtazama Fadhili.

“Mwantumu hebu sema unampenda nani kati yangu mimi na Imran?” Fadhili akahoji kwa jazba akiamini kwa asilimia zote mtoto wa kike ningemchagua yeye.

“Hakuna haja!” Mainaya akaingiklia kati na kuzungumza haraka kwasababu alifahamu jibu langu lingekuwa ni kumchagua Fadhili.

“Kwanini mtu asipewe uhuru wa kuchagua bwana?” Fadhili akahoji kwa msisitizo huku ametoa macho kwa hasira.

“Punguza hasira mdogo wangu, mama naomba umpigie mama yake Tumu azungumze na binti yake. Wajadiliane na watakachoamua basi hatuna budi kukifuata” Mainaya akazungumza kwa sauti ya polepole iliyokuwa imejaa hekima.

“Wala msijisumbue, hata nikizungumza nao hakuna kitakachobalidilika. Sipo tayari kuolewa na kaka Imran” nikazungumza kwa msisitizo kiasi cha kuwafanya wajumbe wa kikao kile hasa dada Mainaya na kaka Imran kuishiwa pozi.

Bi. Fatma hakuongeza neno lolote zaidi ya kutoa simu yake na kumpigia mama yangu kule kijijini kwetu Tanganyika.

“Bi mkubwa unajisumbua bure na kupoteza vocha zako bila sababu. Tumu hawezi kukubaliana na upuuzi huu” Fadhili akazungumza kwa kujiamini.

“Dogo usiusemee moyo wa mtu, wacha wajadiliane na wazazi wake sisi tusubiri majibu tu” kaka Imran akazungumza kwa kujiamini.

“Tatizo kaka Mkubwa unajiamini kupitiliza, lakini huwezi kubadilisha nguvu ya mapenzi” Fadhili akaendelea kuzungumza kwa kujiamini.

“Hebu nyamazeni simu inaita” Mama alizungumza huku akisikiliza simu ile.

Baada ya sekunde kadhaa simu ile ikapokelewa kisha nikapewa kuzungumza na mama.

Ndugu msomaji baada ya kupokea simu ile sikuweza kuamini maneno niliyokuwa nimeyasikia kutoka kinywani mwa mama yangu mzazi Bi. Zamda. Kumbe kaka Imran alikwishafika nyumbani na kujitambulisha huku akifanya mambo makubwa kwa wazazi wangu.

Ndani ya muda mfupi kaka Imran aliweza kuwajengea wazazi wangu nyumba kubwa ya kisasa, Kaka Imran alilima mashamba makubwa kwaajili ya wazazi wangu, bado haikutosha mwanaume huyo akawafungulia duka kubwa sana la jumla na reja reja kwa bidhaa za matumizi ya nyumbani, wengi walizoea kuliita duka la takataka kwasababu kilipatikana kila kitu cha matumizi ya nyumbani.

Kwa kifupi ni kwamba maisha ya wazazi wangu kule kijijini kwetu yalikuwa yameboreshwa kwa kiasi kikubwa na kaka Imran. Yote hayo yalifanyika pasipo mimi kufahamishwa kwasababu alikuwa amekubaliana na wazazi wangu kufanya siri hadi siku ya mwisho.

Maneno ya mama yalimalizika kwa kunisihi huku akiniomba sana nisije nikamuangusha kwa kukataa kuolewa na kaka Imran. Waliniomba sana nisije nikamsaliti kaka Imran na kutembea na mwanaume mwingine. Wakazidi kusisitiza kuwa kutokana na utu uzima waliokuwa nao waliweza kubaini mapenzi ya dhati aliyokuwanayo kaka Imran juu yangu.

Nilimsikiliza sana mama ambaye alifikia hatua ya kuzungumza kwa hisia kali kiasi cha kuanza kulia. Nilishindwa kuzungumza neno lolote lile Zaidi ya kububujikwa na machozi kwenye mashavu yangu. Kusema ukweli nilikuwa nikiwapenda sana wazazi wangu na nilikuwa tayari kufanya chochote kile ilimradi wazee wale waishi katika mazingira yaliyojaa Amani na furaha.



Niliogopa sana na kuhisi kama ningekataa kuolewa na kaka Imran ambaye kwao alikuwa ni chanzo cha faraja hata Mwenyezi Mungu asingenisamehe.

Simu ilikatika lakini bado nilikuwa nimeganda nayo sikioni kama vile nimegundishwa kwa superglue.

“Vipi mama umemaliza?” nikagutuka na kunyoosha mkono kumkabidhi mama ile simu. Kila mtu ndani alikuwa kimya akisubiria kwa makini maamuzi ambayo ningeyatoa.

“Naomba ukate huu mzizi wa fitina Tumu” Bi. Fatma akazungumza kwa msisitizo mkubwa kwasababu wote wale walikuwa ni watoto wake hivyo yeyote yule ambaye ningemchagua yeye angekubaliana nami.

Niliinua macho yangu na kumuangalia kaka Imran usoni kwa makini. Sikuwezakuamini kwa jinsi nilivyokuwa nikimchukulia kama mtu mmoja katili na mkorofi sana. Sikuwahi kufikiri hata siku moja kama angekuwa ni mwanaume mwenye roho ya huruma kiasi kile na kufanya mambo makubwa kwa wazazi wangu. Nikang’amua kuwa kumbe kaka Imran alikuwa akinipenda kwa dhati kabisa.

Niligeuza shingo na kumtazama Fadhili ambaye alikuwa ameketi kwa kujiamini akiwa na uhakika kwa asilimia zote kuwa ningemchagua yeye hasa ukizingatia ni yeye ambaye nilimkabidhi usichana wangu na ni yeye aliyeniingiza kwenye ulimwengu wa mapenzi kwa mara ya kwanza.

“Nisamehe sana Fadhili” nikazungumza kwa uchungu na kuzidi kumwaga machozi.

“Unataka kusemaje Mwantumu?” Fadhili akahoji kwa mshituko baada ya kusikia ile kauli yangu.

“Basi biashara imekwisha!” Dada Mainaya akazungumza huku akimtazama kaka Imran kwa tabasamu la ushindi.

“Nambie tu Mwantumu wala usiogope!” Fadhili akazungumza kwa kuchachawa.

“Sio mimi Fadhili ni wazazi wangu” nikazungumza kwa uchungu huku nikilia.

“Huo ni usaliti Mwantumu, usikubali kutenda hiyo dhambi” Fadhili akazungumza kwa kusihi huku akionekana kuchanganyikiwa.

“Sina jinsi Fadhili ni lazima niolewe” nikazungumza kwa masikitiko makubwa.

“Kama ni suala la ndoa hata mimi nitakuoa tu” Fadhili akazungumza kwa kubembeleza kiasi cha kuzidi kuniongezea uchungu ndani ya moyo wangu.

“Fadhili mwanangu, inabidi tukubaliane na matokeo, huwezi jua Mungu amekuepushia kitu gani huko mbeleni” Mama akazungumza kwa sauti ya kufariji ili kumtia moyo Fadhili.

“Hapana mama tusipeane moyo kinafki. Haya ambayo mmenifanyia ni ukatili mkubwa sana” Fadhili akazungumza kwa jazba.

“Dogo, umesahau dakika mbili zilizopita ulikuwa unapondea mapenzi ya lazima, sasa imekuwaje?” Kaka Imran akazungumza kwa kejeli huku akikonyezana na Binamu yake Mainaya.

“Ndoa za kulazimishana ziliishia kwenye kitabu cha Damu ya Kibena” alisema dada Mainaya kwa vijembe.

“Nyie ndio mnalazimisha mapenzi na sio mimi” Fadhili akazungumza kwa ukali.

“Nani tena analazimishwa kuolewa humu ndani ya nyumba yangu!” sauti ya Baba ilitugutusha na kugeuza shingo zetu kumuangalia. Alikuwa amesikia lile neno la dada Mainaya la kwamba ndoa za kulazimishana akaamini mimi ndiye niliyekuwa nikijadiliwa.

“Nafikiri sijachelewa sana” Baba alizungumza huku akijiweka kwenye kochi alilokuwa ameketi mke wake.

“Karibu mume wangu umefika muda muafaka” mama akajibu kwa ufupi.

“Mbona kuna kulazimishana ndoa tena!” Baba akahoji huku akiamini jibu la swali lake lingefungua njia ya yeye kunioa mimi kama mke wa pili. Alikuwa amepania kutumia kikao kile kuhakikisha mpango wa kaka Imran wa kunioa mimi unavurugika na badala yake lengo lake la kunifanya mimi kuwa mke wake wa pili linasimama na kufanikiwa.

“Taratibu basi mume wangu, utafahamishwa kila kitu” mama akazungumza kwa sauti ya upole.

“Tangu nipo nje nasikia ndoa ya lazima, ndoa ya lazima! Ndiyomaana nataka kufahamu ni nani anayelazimishwa ndoa? Maana siku hizi hakuna ndoa za lazima” Baba akazungumza kwa msisitizo mkubwa huku ametoa macho.

“Baba wasikuzunguushe, wanamlazimisha Tumu kuolewa na kaka Mkubwa” Fadhili akazungumza kwa msisitizo na jazba kubwa.

“Ni mshenzi gani huyo anayejaribu kufanya mambo ya kifirauni hayo ndani ya nyumba yangu?” Baba akahoji kwa hasira za kujilazimisha huku akiamini kuwa lengo lake lilikuwa linaelekea kutimia.

“Hapa hakuna ndoa ya lazima baba, muulizeni tena Tumu aseme anampenda nani!” kaka Imran akazungumza kwa kujiamini huku akihisi zoezi lake limeanza kupata tena kipingamizi kutoka kwa Baba.

“Tumu mwanangu, naomba ueleze ukweli kutoka moyoni. Unampenda nani?” mama akahoji kwa msisitizo akiwa na lengo la kumaliza mvutano ule na kufuta kabisa matumaini ya Baba ya kunifanya kuwa mke wa pili.

“Mimi ninalo jibu la swali hilo” Baba alidakia haraka sana kwa kuhofia kuwa ningemtaja mtu mwingine kabisa tofauti na yeye. Alitaka kutumia mwanya ule kueleza hisia zake juu yangu na lengo lake la kunifanya kuwa mke wa pili lakini mama akapuuza haraka sana.

“Tunataka ajibu mwenyewe” mama akasisitiza.

“Jibu Tumu…Jibu haraka!” Fadhili akazungumza kwa msisitizo.

“Mimi nitaolewa na kaka Imran, nisamehe sana Fadhili” nikazungumza kwa sauti ya msisitizo huku nikiamini kama nikiendelea kubembelezana na Fadhili pale mambo yangezidi kuniwia magumu.



“Unasemaje we mtoto?” Baba akahoji kwa kuhamaki.

“Mwenye masikio na asikie na mwenye macho na atazame. Biashara imeisha namna hiyo. Tuangalie utaratibu wa ndoa na sherehe umekaaje” dada Mainaya akazungumza kwa furaha kubwa maana upande wake ulikuwa umeshinda kwa kishindo.

“Swala hilo haliwezekani” alizungumza Baba kwa msisitizo.

“Kwanini tena Mjomba?” Mainaya akahoji kwa mshangao mkubwa.

“Inamaana Bi. Fatma umesahau nilipokueleza kuwa….” Baba aliataka kufunguka kila kitu juu ya hisia zake kwangu mbele ya watoto wake lakini mama akamuwahi na kumzuia.

“Ishia hapo hapo! Neno moja tu la ziada litachafua heshima yako milele daima” alizungumza mama kwa msisitizo na tahadhari kubwa.

Maneno ya mama yalionekana kumuingia vyema Baba na kuhisi ukweli wa jambo hilo. Kama kweli angeeleza pale kuwa alikuwa anataka kunioa mimi basi ni lazima watoto wake wangemshushia heshima na kumdharau hasa ukizingatia watoto wenyewe walikuwa katika mgogoro kutokana na mimi. Hivyo mzee yule hakuwa na namna Zaidi ya kukubaliana na matokeo na kusimama kama Baba wa familia.

Fadhili alijikuta akiishiwa nguvu na hakuelewa ni kitu gani kilikuwa kimenikumba wakati ule. Alikuwa kama vile msukule aliyebahatika kurudi tena katika maisha ya duniani. Alishindwa kuhoji wala kulaumu na badala yake akawa ameganda utafikiri amekaushwa na shoti ya umeme. Alianza kuamini kuwa uchawi ulitumika kubadilisha akili yangu. Isingewezekana hata kidogo kwa mapenzi niliyokuwa nikiyaonyesha kwake muda mfupi uliopita yangeweza kuyeyuka ghafla kiasi kile.

Sikuweza kumuangalia Fadhili usoni mara mbili, nilihisi maumivu makali sana moyoni huku nafsi ikinisuta kutokana na usaliti niliokuwa nimemtendea kijana yule. Sijui kama ni kweli ulikuwa ni usaliti lakini sikuwa na namna niliwapenda sana wazazi wangu kuliko kitu kingine chochote kile chini ya jua.

Nilimuona Fadhili akijiinua kwa unyonge sana kutoka pale alipokuwa ameketi na kuvuta hatua kuondoka akituacha na kikao chetu. Nilishindwa kuvulimia ndugu msomaji, niliinuka na kumfuata mbio.

Kaka Imran naye aliponiona nimeinuka kumfuata Fadhili na yeye akainuka ghafla kutaka kunifuata kwa nyuma akihofia Fadhili angeweza kufanya mapinduzi kwa kutumia nguvu ya penzi.

“Hapana Imran tulia. Unatakiwa kufahamu hali aliyokuwa nayo mdogo wako, tusipokuwa makini tunaweza kusababisha matatizo makubwa sana katika hii familia” mama alimzuia kaka Imran na kueleza maneno hayo. Kama Imran alitii maneno ya mama yake na kuketi kwenye kochi.

“Ni kitu gani kinaendelea humu ndani?” Baba akahoji kwa mshangao kwasababu hakuwahi kufikiria kama Fadhili naye alikuwepo kwenye msafara wa kuwania penzi langu.

“Mume wangu, haya mambo ni mazito mno” mama alizungumza na kumeza mate.

“Endelea nakusikiliza” Baba akasisitiza.

“Watoto wako wote wameangukia kwenye penzi la Mwantumu” mama alizungumza kwa msisitizo akielewa hata Baba naye alishamwambia kuwa ananipenda.

“Iinawezekanaje jambo hilo?” Baba akajifanya kushangazwa na kile kitendo cha wanaume wawili kumpenda binti mmoja.

“Mwenyewe unamuona Mwantumu alivyokuwa mrembo, hakuna mwanaume yeyote yule ambaye atamuona halafu ashindwe kumtamani. Labda mwanaume huyo awe na tatizo la kimaumbile” mama alizungumza maneno yale akiwa na maana ya kwamba hata baba naye alikuwa ni miongoni mwa wale wanaume waliokuwa wamedondokea kwenye penzi la binti wa kitanga.

“Unataka kusema mimi sio mwanaume?” Baba kahoji kwa mshangao kutokana na kauli ile ya mke wake.

“Hata wewe ni mwanaume mume wangu!” mama alijibu kwa ufupi.

“Kwahiyo na mimi ninamtaka huyu mtoto?” Baba akajifanya kuhoji kwa hasira na mshangao.

“Umeninukuu vibaya mume wangu, ninamaanisha hawa watoto” mama akazungumza maneno yale huku akihisi mkakati wake wa kupinga mpango wa baba kunifanya kuwa mke wake wa pili ulikuwa umefanikiwa.

“Nilidhani na mimi unanifananisha na hawa panya wako” Baba alizungumza akijiweka vizuri kwenye kochi huku ndani ya nafsi yake akilaani kila kitu kilichokuwa kikiendelea pale.

Kule nilipokuwa nimemfuata Fadhili nilikuwa nikitembea kwa hatua za haraka huku machozi yakinitoka.

“Fadhili..” nikaita kwa sauti ya kukata kata.

“Unasemaje” aliitika Fadhili kwa jazba baada ya kugeuka na kuniona nikimfuata.

“Nisamehe Fadhili kwahili” nikazungumza kwa kubembeleza.

“Hivi ni wewe Tumu ninayemfahamu mimi au nipo ndotoni?” Fadhili alizungumza kwa hisia kali.

“Kama kweli mimi ni wako naamini siku ya mwisho tutafufuliwa tukiwa pamoja na tutaishi pamoja katika uzima wa milele” nikazungumza huku nikilia kwa uchungu.

“Wacha unafki wako we mwanamke! Yaani kweli unanikana hadharani? Nimeamini wanawake ni nyoka!” Fadhili akazungumza kwa uchungu mkubwa na kuzidi kunitengenezea maumivu ndani ya nafsi yangu.

“Usiseme hivyo Fadhili unaniumiza ujue!” nikazungumza kwa kulalamika.

“Unajua kuumia wewe au unaropoka kinafki tu?”

“Nakupenda Fadhili tafadhali tambua hilo” nilizungumza kwa msisitizo na kujaribu kumshika mkono wake wa kulia.

“Hebu achia mkono wangu! Kama kweli unanipenda usingeweza kufanya mambo kama haya” alizungumza kwa hasira Fadhili huku akitetemeka. Kwa mara ya kwanza niliweza kumuona Fadhili akiwa katika hali kama ile.

“Sio mimi Fadhili, wazazi wangu ndio wananilazimisha niolewe na kaka Imran” nikajaribu kueleza pengine angenielewa.

“Wazazi hawana nguvu katika mapenzi, tafadhali bado nimekuopa nafasi ndani ya moyo wangu” Fadhili alijaribu kunisihi na kunibembeleza.

“Hapana Fadhili, wazazi wangu nimewapa nafasi ya kuniamulia kwa kila jambo” nikaeleza.

“Hunipendi na ndiyomaana unazungumza mautumbo utumbo yako hapa” alizungumza kijana yule kwa jazba.

“Usijali, mimi ninaamini utapata mwanamke mwengine mzuri kuliko hata mimi” nikajaribu kumfariji lakini mambo yakawa tofauti kwasababu Fadhili alizidi kupandwa na hasira.

“Nyie wanawake watu wabaya sana, sijui kama kuna mwanamke hata mmoja ambaye atauona ufalme wa mbingu” Fadhili alizidi kuzungumza maneno machachu masikioni mwangu.



“Usiseme hivyo Fadhili..” nikazungumza na kumsogelea kutaka kumkumbatia.

“Toka hapa..!” alizungumza kwa sauti kubwa ya ukali na kunisukuma kwa nguvu. Nilipepesuka da kudondokea ukutani.

“Wee…Weee..weee… Cheza mbali na wake za watu! Kwanini unamsukuma mke wangu kiasi hicho?” kaka Imran alishuhudia kitendo kile alichokuwa amenifanyia Fadhili cha kunisukuma kwa hasira.

“Ongea na malawa wako asitamani shemeji zake!” Fadhili naye akazungumza kwa kebehi huku akigeuka kuondoka.

“Unamuita Malaya mke wangu? We dogo angalia sana!” alizungumza kaka Imran huku akininyanyua kutoka pale nilipokua nimedondokea na kunikumbatia.

“Umeumia mchumba?” alihoji kaka Imran kwa sauti ya upendo iliyoonesha kujali.

“Hapana..” nikajibu kwa shida.

“Kaa mbali na Fadhili, yule sio mtu mzuri” kaka Imran alizungumza na kunipiga busu lakwenye paji la uso kisha akanikumbatia kwa nguvu. Nafikiri alikuwa akiisubiria kwa hamu kubwa sana nafasi kama ile. Hatimaye mtoto wa kike nikajikuta kwenye mikono ya kaka Imran mwanaume ambaye sikuwahi kutamani kuishi naye kama mke na mume.

*****

Kutokana na hali halisi iliyokuwepo pale nyumbani kwa mzee Sekiza ilibidi wanirudishe nyumbani Tanganyika kwaajili ya maandalizi ya harusi. Pamoja na kwamba nilikuwa nikijitahidi sana kumsahau Fadhili lakini ilikuwa ni ngumu mno. Mara kadhaa nilipokuwa peke yangu macho yalinitoka huku nafsi yangu ikijuta kwa kitendo nilichokuwa nimemfanyia mpenzi wangu Fadhili.

Faraja pekee niliyokuwa nikiipata ni maisha bora waliyokuwa wakiishi wazazi wangu kutokana na misaada waliyokuwa wameipata kutoka kwa mchumba wangu Imran. Hakika nilikuwa nikimuombea dua kwa Mungu azidi kumbariki mwanaume yule. Ni wanaume wachache sana katika ulimwengu wa leo ambao wanajali na kuthamini maisha ya familia za wake zao.

Kwa upande wa Fadhili nako mambo yalikuwa ni magumu mno. Hakutegemea mwanamke aliyekuwa akimpenda na kufanya kila aina ya mbinu kuhakikisha anakuwa naye karibu anabadilika na kumwaga hadharani bila hata ya huruma.

Hata hivyo hakuwa na namna yoyote ile kijana wa watu. Kikubwa ambacho alikifanya ni kufanya sana ibada na kumuomba Mungu ampatie ujasiri na moyo wa hekima ili jambo lile lisijekufika hatua mbaya zaidi na kupelekea matatizo katika familia yake.

Pamoja na kwamba alipata shida sana kukubaliana na matokeo yale lakini hatimaye akajilazimisha na kwa kiasi fulani akawa sawa. Naweza nikasema mwenyewe alikuwa anajipa moyo na kujiona kuwa sawa lakini ukweli ulibakia palepale kidonda cha mapenzi kiliendelea kumtesa.

Maandalizi ya Harusi yaliendelea kwa spidi ya mwendo kasi. Ndani ya mwezi mmoja na nusu tayari kila kitu kilikuwa kimekamilika na hatimaye tarehe ya harusi ikafika. Sherehe zile zilipangwa kufanyika kijijini Tanganyika nyumbani kwa mama Kibo yule dada yake Bi. Fatma ambaye alitumia nguvu nyingi sana kunishawishi niolewe na kaka Imran lakini juhudi zake ziligonga mwamba. Hata hivyo furaha yake ilirejea upya baada ya kubaini mipango ya ndoa ile ilikuwa palepale.

Nakumbuka nilikuwa kwenye chumba cha bibi harusi nimeketi kitandani huku pembeni mwangu alikuwepo somo akiendelea kuniweka sawa kila idara. Hakika mtoto wa kike nilikuwa nimependeza kuliko kawaida. Kila mwanamke akirembwa huwa ni mrembo lakini mimi mwenzenu nilipitiliza na kuwa kama vile malaika.

Yalikuwa yamesalia masaa machache tu kwaajili ya mimi na mchumba wangu Imran kufunga ndoa. Ghafla kumbukumbu za Fadhili zikanijia ndani ya ubongo wangu na kunifanya ninyong’onyee kidogo na kupoteza nuru kwenye sura yangu. Nilitamani kama ningeweza ningeonana angalau kidogo tu na Fadhili, nimpige busu na kumkumbatia kwa nguvu kisha nimwambie kuwa NAMPENDA. Hata hivyo ilikuwa ni kama mipango ya kujenga ghorofa angani bila ya kuweka nguzo aldhini. Nisingeweza kufanya yote hayo kwa kijana yule niliyekuwa nimempenda kwa dhati kutoka moyoni.

Sauti za chereko chereko na vigeregere zilinipa ishara ya kwamba Bwana harusi alikuwa amefika nyumbani pale tayari kwa ndoa. Nilihisi mapigo ya moyo yakinienda mbio lakini nikamuomba Mungu aweze kunipa ujasiri. Kwa bahati mbaya ama nzuri nilipoinua macho yangu niliweza kumuona Bwana harusi na msimamizi wake kupitia dirishani.

Nilishituka sana na sikuweza kuamini macho yangu. Msimamizi wa bwana harusi alikuwa ni Fadhili. Mwanaume ambaye alikuwa akisumbua akili yangu kwa muda mrefu.

Nilitamani kusimama na kwenda kuhakikisha nilichokiona lakini kwakuwa nilikuwa ni Bibi harusi sikuweza kufanya yote hayo. Nikatamani Bwana harusi na msimamizi wake wapite tena usawa wa dirisha langu ili niweze kuthibitisha uwongo wa macho yangu lakini dua yangu haikujibiwa na badala yake nikaambulia kuwaona watu wengine waliokuwa wakisherehekea ndoa ile wakipita pita.

Bwanaharusi na wasimamizi wake walikaribishwa na kuketi sebleni kwenye mkeaka tayari kwa ibada ya ndoa.

Kule chumbani nilipokuwepo walikuja mashahidi kutoka upande wa Bwana harusi pamoja na mashahidi kutoka upande wa Bibi harusi. Lengo lilikuwa ni kupata uthibitisho kama ni kweli nilikuwa nimeridhia ndoa ile kutoka ndani ya nafsi yangu mwenyewe pasipo kulazimishwa na mtu yeyote.

Kabla ya kuhojiwa jambo lolote lile nilianza kuhisi tumbo likinikoroga na kunivuruga. Kichefuchefu kikali kikanivaa na kujikuta nikitapika bila kutegemea. Nilipata msaada kutoka kwa mashahidi wale wa pande zote mbili na baada ya muda kidogo nikakaa sawa.

“Somo..unaweza kuwa na lolote la kuzungumza?” Mwanamke mmoja kutoka upande wa mashahidi wa bwana harusi alihoji.

“Kijana wenu hakuwahi kukutana na binti yetu, nafikiri ni hofu tu” somo wangu alizungumza kwa lugha ya kiufundi.

“Hapana, tunakupa nafasi uzungumze vizuri na binti” mwanamke yule alizungumza huku akiwapa ishara wenzake kutoka chumbani mle na kubaki mimi, somo wangu pamoja na somo wa Bwana harusi.

“Mwantumu mwanangu, naomba uniambie ukweli ili nijue namna ya kukusaidia” alizungumza somo wangu sauti ya kubembeleza.

“Ulishawahi kukutana na Imran hata mara moja?” Somoye Imran alihoji.

“Hapana…” nikakataa huku nikitikisa kichwa.

“Kuna mwanaume yeyote ambaye ulikutana naye hivi karibuni?” Somo yangu alihoji.

Sikuweza kutoajibu la swali lile kwasababu kwa upande wangu nililiona kama vile lilikuwa ni tusi.



“Naomba usiogope, tuanataka kukusaidia” somoye Imran alizungumza kwa msisitizo.

“Ndio..” nikajibu kwa ufupi baada ya kuona wananibananisha mno.

“Muda gani umepita?” alihoji somo yangu kwa umakini mkubwa.

“Kama mwezi hivi..”nikaeleza.

“Tangu ukutane naye ulishawahi kusafiri mkoani?” Somo yangu akahoji.

“Hapana…” nikajibu.

“Kwahiyo wewe ni mjamzito si ndivyo?” Somoye Imran alihoji kwa msisitizo na kunifanya nishituke kidogo. Sikutegemea kusikia kauli kama ile kwenye siku yangu ile muhimu. Nikabaki nimekodoa macho nisijue la kuzungumza.

Ndugu msomaji sikuweza kufahamu majibu yangu yalikuwa ni ya kujichoma mwenyewe. Zoezi lile la ndoa lilisitishwa kidogo huku kwa siri kubwa sana vililetwa vipimo vya mimba mlemle chumbani na kupimwa mkojo kama kweli nilikuwa nimesalimika na lile walilokuwa wakilihisi wao.

Wakati mwingine Mungu akiamua kutokuwa upande wako hata ufanye nini mambo hayaendi kama unavyotaka wewe. Niliomba sana huku nikisoma dua mbalimbali nikiepuke kikombe kile cha dhambi lakini Mungu hakuwa upande wangu siku hiyo. Majibu ya vipimo yalionesha kuwa nilikuwa ni mjamzito.

Ndugu msomaji ndoa ikabadilika na kuwa ndoano, nakwambia ikawa pata shika nguo kuchanika. Hata hivyo jambo la kumshukuru Mungu ni kwamba mambo yote yale yalikuwa yakiendesha baina ya ndugu wa pande mbili pasipo watu wengine kubaini kilichokuwa kinaendelea.

Dada Mainaya alikwenda kupiga goti nyuma ya Imran na kumnongo’neza kwa kumueleza kuwa kulikuwepo na tatizo kubwa hivyo alimuomba wazungumze kidogo pembeni. Pasipokuleta pingamizi wala ubishi Bwana harusi aliinuka na kumfuata Mainaya pembeni.

“Kuna tatizo gani mbona siwaelewi humu ndani?” alihoji Bwana harusi kwa wasiwasi.

“Kuna tatizo mdogo wangu na ndiyomaana unaona mambo yanachukua muda” alizungumza Mainaya kwa umakini.

“Tatizo gani, Mke wangu anaumwa?” Alihoji Imran kwa hofu na mashaka.

“Ndio..” Mainaya akajibu kwa ufupi.

“Mungu wangu, yuko wapi?” Bwana harusi alihamaki na kutaka kwenda kule chumbani kuniona.

“Ngoja kwanza” Mainaya alimzuia kwa kumdaka mkono kaka Imran.

“Sasa dada Mainaya kama mtu anaumwa si inabidi apewe msaada” alizungumza kaka Imran kwa hofu.

“Usihofu, Tumu ameshasaidiwa” Mainaya akazungumza kwa upole.

“Anaendeleaje kwa sasa?”

“Yupo sawa kabisa”

“Mungu ni mwema!” alizungumza Bwana harusi huku akifuta jasho.

“Sikiliza mdogo wangu, ni lazima ujikaze” Mainaya akazungumza kwa sauti ya upole.

“Kwani kuna nini sister?” Imran akahoji kwa hofu.

“Naomba utulie mdogo wangu” Mainaya akazungumza kwa sauti ya upole.

“Naomba usinizunguushe Binamu, nieleze ni kitu gani kinaendelea huko ndani?” Imran akahoji kwa kuchachawa.

“Mwantumu ni mjamzito” Mainaya akazungumza kwa msisitizo.

“Mungu wangu!” kaka Imran akashituka sana baada ya kupokea taarifa ile kutoka kwa dada Mainaya. Lishika kichwa na kujizunguusha mara tatu kama pia.

“Naomba ujikaze Imran”

“Inawezekanaje hii, Binamu inawezekanaje?” Masikini kaka Imran akahoji kwa Hasira huku akionekana kuchanganyikiwa.

“Sikiliza Imran, wakati tunamchukua Tumu kutoka kwa Fadhili, tayari walikuwa wameshakutana” Mainaya alizungumza kwa msisitizo.

“Kwahiyo ushenzi huu amefanya Fadhili?” Bwanaharusi akahoji kwa hasira.

“Sio kwamba amefanya kaka, sisi ndio tumemfanyia ushenzi” alizungumza Mainaya maneno ambayo alihisi yangerudisha hali ya Bwana harusi kuwakawaida.

“Unataka kusemaje?” Akahoji kaka Imran huku akihisi dunia inazunguuka.

“Ulishawahi kulala na Tumu hata siku moja?” Mainaya akahoji.

“Hapana..”

“Basi kaka mkubwa lazima ukubaliane na matokeo” Mainaya alizungumza.

“Inamaana nimuoe mtu mwenye ujauzito wa mwanaume mwengine?” kaka Imran akahoji kwa kuhamaki.

“Ni lazima ufanye hivyo”

“Haiwezekani!”

“Kinyume na hivyo mwenye ujauzito wake ndio aoe” Mainaya akazungumza kwa msisitizo mkubwa.

“Nitamuoa mwenyewe lakini ujauzito inabidi utolewe” Imran akazungumza.

“Hapana kaka Mkubwa, kutoa mimba ni dhambi kubwa sana. Angalia namna tofauti ya kufanya” Mainaya alizungumza.

“Kama ni hivyo, ni bora waoane wenyewe wenye mimba yao” kaka Imran akazungumza kwa hasira.

“Safi huo ni uamuzi wa busara, vinginevyo tutaingia kwenye kashfa kubwa sana” Mainaya akazungumza kwa msisitizo.

Wakati Mainaya alipokuwa kizungumza na Bwana harusi, Fadhili akahisi hali tofauti katika shughuli ile. Alijiinua kutoka pale kwenye mkeka na kuwafuata pale walipokuwa wamesimama.

“Jamani kuna usalama kweli?” Fadhili akahoji kwa mashaka.

“Usalama upo lakini mambo yamekwenda kinyume na mpangilio” dada Mainaya akazungumza kwa sauti ya upole iliyokuwa imepoteza matumaini.

“Imekuwaje kwani?” Fadhili akahoji kwa msisitizo mkubwa.

“Kuanzia hivi ninavyozungumza wewe ndiye Bwana harusi na mimi ndiye msimamizi wako” kaka Imran alizungumza huku akivua kiremba na kumvalisha Fadhili ambaye hakuwa anaelewa kilichokuwa kikiendelea kwa wakati ule.

“Kwani imekuwaje Binamu?” Fadhili alihoji huku kaka Imran akiendelea kumvalisha kiremba cha bwana harusi.

“Bibi harusi ana ujauzito wako” alisema Mainaya kwa kifupi.

“Unasemaje?” Fadhili akahoji kwa mshituko.

“Bibi harusi anatarajia kupata mtoto wako” Mainaya akaeleza kwa msisitizo.

“Inawezekanaje?” Fadhili aliendelea kushangazwa na habari ile.

“Katika ulimwengu wa leo inawezekana!” kaka Imran akazungumza kwa ufupi.

“Lakini mimi nilisha achana naye tangu siku ulipotambulisha wazo lako” Fadhili akajaribu kuzungumza kwa kujitetea.

“Wakati unamuacha ulikuwa umeshakutana naye?” Dada Mainaya akahoji kwa msisitizo huku akiwa anaufahamu ukweli wote kwasababu siku hiyo alinikamata nikitokea chumbani mwa Fadhili.

“Lakini dada Mainaya…”

“Hakuna cha lakini Fadhili, toa jibu” Mainaya akasisitiza.

“Nilikutana naye mara moja tu” Fadhili akaropoka pasipo kutegemea.

“Sasa mkutano wenu umezaa matunda, leo inabidi ufunge ndoa na mama kijacho wako” alizungumza Mainaya kwa msisitizo.

“Fadhili mimi sina kinyongo na wewe, najua mimi ndiye niliyevuruga mahusiano yenu. Tafadhali naomba ukubali kufunga ndoa na Mwantumu” Kaka Imran akazungumza kwa msisitizo mkubwa.

“Lakini si mnafahamu kwamba haiwezekani?” Fadhili akazungumza kwa hofu.

“Itawezekana tu” kaka Imran akasisitiza.

“Hii ndoa haitaswihi. Mbele za Allah ni batili na hukumu yake ni nzito mno” Fadhili akazungumza kwa msisitizo.



“Kwanini tubishane wakati watu wazima wapo, nafikiri na wao wanamaono yao pia. Ni vyema tuwasikilize” dada Mainaya alizungumza na kumaliza ule mvutano uliojitokeza katika akikao kile cha dharura.

Mambo yalizidi kuwa magumu kadri muda ulivyosonga mbele. Hali ya sinto fahamu ilikuwa imetawala kwa wanandugu wa pande zote mbili. Haraka sana ilibidi kikao cha dharura kwa pande zote mbili kiitishwe. Wakajifungia kwenye chumba ambacho kilikuwa na utulivu.

“Jamani mambo ndio kama haya yanavyoonekana, sasa tunafanya nini?” alizungumza baba yangu mzazi mzee Mudy.

“Maadam bwana harusi yupo hapa, tumpe nafasi” Bi. Fatma alizungumza kwa ufupi huku akionekana kuchanganyikiwa kutokana na mambo yale.

Maneno ya Bi. Fatma yaliweza kumfanya kila mtu chumbani mle kupeleka macho yake kumtzama kaka Imran ambaye kwa wakati ule alikuwa ameshavua mavazi kama bwana harusi na kumvalisha Fadhili.

“Kijana tunakusikiliza” mzee Mudy alihoji baada ya kumuona kaka Imran yupo kimya.

“Kwanza kabisa ningependa kuomba radhi na msamaha kutoka kwa mdogo wangu Fadhili, wazazi wangu pamoja na wazazi wa Mwantumu” kaka Imran alizungumza kwa sauti ya unyenyekevu kisha akavuta pumzi na kuzitoa kwa nguvu.

“Kwanini unasema hivyo?” mama Kibo ambaye naye alikuwepo kwenye kikao hicho alihoji.

“Mimi pamoja na dada Mainaya tuliweza kufanya kila hila kuhakikisha tunapora penzi la Mwantumu kutoka kwenye moyo wa mdogo wetu Fadhili” kaka Imran alizungumza taratibu na kwa msisitizo mkubwa.

Kila mmoja kwenye kikao kile aliketi vizuri kuweza kusikiliza kwa makini maelezo yale kutoka kwa Bwana harusi kaka Imran.

“Kila jambo jema ambalo niliwafanyia wazazi wa Mwantumu lengo langu lilikuwa ni kutengeneza ushawishi kuhakikisha biti yenu anakuwa na mimi. Lakini ukweli ni kwamba binti yenu anampenda zaidi mdogo wangu Fadhili” Kaka Imran alizungumza kwa uchungu na majuto makubwa.

“Kwahiyo unataka kusemaje?” Baba yangu mzazi mzee Mudy alihoji. Hakutaka kuendelea kusikia jinsi ambavyo walifanywa wapumbavu kwaajili ya penzi la binti yao.

“Ningeomba siku ya leo, mdogo wangu Fadhili afunge ndoa na Mwantumu badala ya mimi” kaka Imran akazungumza kwa msisitizo huku akionekana kuridhia kwa tukio hilo.

“Unapanga tu pasipo kufikiri, unadhani kila unalolitaka wewe ni sahihi?” mzee Mudy akahoji kwa jazba kidogo.

Muda wote huo Fadhili alikuwa amejiinamia kimya utafikiri mateka wa vita vya pili vya dunia. Alijaribu kutafakari jambo lakini hakuelewa hata jambo lenyewe alilokuwa analitafakari.

“We kijana unasemaje mana umedhihirisha uanaume wako kwa kumjaza upepo biti yetu nje ya ndoa” mzee Mudy alizungumza na kumgutusha Fadhili kutoka kwenye yale mawazo yake yasiyoeleweka.

“Naam..” Fadhili akaitika kama vile hakuwa amesikia swali la Baba yangu mzazi.

“Umeyasikia maneno ya nduguyo?” mzee Mudy alihoji.

“Ndio..”

“Haya tueleze mipango yako” mzee Mudy akahoji.

“Kusema kweli, mimi ninampenda sana Mwantumu.Lakini siwezi kufunga ndoa na binti yenu” Fadhili akazungumza kwa msisitizo.

“Kwahiyo wewe hutaki kumuoa binti yangu pamoja na kwamba umesha mtundika mimba, na wewe hutaki kumuoa binti yangu pamoja na kwamba umesha andaa taratibu zote na kuutangazia ulimwengu kuwa unamuoa. Hivyo mnataka kumuweka katika wakati gani mtoto wangu?” mzee Mudy akazungumza kwa jazba.

“Mimi sijakataa mzee kumuoa binti yako, tatizo dini” Fadhili akazungumza.

“Dini imefanya nini au wewe ni Mgalatia?” alihoji mzee Mudy kwa umakini mkubwa.

“Kwakuwa Shekh yupo hapa, nafikiri angezungumzia hukumu hii. Kama itaswihi basi nitakuwa tayari kufunga ndoa na binti yenu hata sasa hivi” Fadhili akazungumza kwa msisitizo na maelezo ambayo yalieleweka kwa kila mtu ndani ya chumba kile.

“Shekh Karibu utueleze lolote juu ya jambo hili” mzee Mudy ambaye kwenye kikao hicho alisimama kama mwenyekiti alimkaribisha Shekh kutoa maelekezo kwa jamii ile.

“Jambo la kwanza ambalo tunafaa kuelewa ni kuwa zinaa ni kitendo kibaya sana kilichokatazwa na Allah (Subhaanahu wa Ta'ala) na Mtume Wake (Swalla Llaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Na yeyote mwenye kufanya amali hiyo basi angefaa apatiwe adhabu ya kisheria” Shekh yule alizungumza kwa lafudhi yake ya kiislamu ambayo mashekh wengi wanaitumia wanapozungumza masuala ya dini.

“Shekh unaweza kuzungumzia moja kwa moja tatizo ambalo linatukabili” baba Mzee Sekiza akavunja ukimya na kutoa ushauri kwa kiongozi yule wa dini.

“Tumpe nafasi aeleze mzee Mwenzangu, Shekh endelea” alizungumza baba mzee Mudy.

“Mwanamke hawezi kuolewa akiwa ana mimba mpaka azae kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza kumwaga mbegu za uzazi juu ya mbegu nyengine” Shekh yule alizungumza na kumeza mate.

“Kwahiyo ndoa ni baada ya Binti kujifungua?” alihoji mzee Sekiza kwa umakini mkubwa.

“Baada ya mwanamke kujifungua, wanaweza kuoana ila kama wote watakuwa wamefanya toba ya kweli kabisa” Shekhe alifafanua.

“Na vipi kwa wanazuoni wanaosema kuwa watu hawa hawataruhusiwa kuoana hata baada ya kufanya toba?”Baba mzee Mudy akahoji kwa umakini mkubwa.

“Huu ndio msimamo sahihi (Wa Allahu A'alam) kulinganisha na ule wa wale wanaokataza wasioane hata baada ya toba. Matokeo yake watu wanaendelea kufanya zinaa maadam wamependana na hawawezi kuwa mbali” alizungumza shekh yule kwa msisitizo.

“Kwa maana hiyo Baba mwenye mtoto ndiye atakayepaswa kufunga ndoa na binti” kaka Imran akazungumza kwa msisitizo huku akionekana Dhahiri kujutia maamuzi yake ya kulazimisha kunioa mimi.

“Laa hasha! Kishariy’ah kwa mujibu wa Wanazuoni wengi, huyu mtoto anayezaliwa akiwa ni msichana au mvulana si wa baba na akiwa ni wa kike baba huyo wa kidamu hawezi kutoa idhini ya kumuozesha.” alizungumza Shekh kwa msisitizo.

“Kwa mujibu huo Shekh, unataka kutuambia kuwa mtoto atakayezaliwa sio damu yetu?” Bi. Fatma naye akatupia swali kwa umakini mkubwa.

“Ukweli upo hivyo ijapokuwa baadhi ya Wanazuoni wanaonelea kuwa mtoto atakayezaliwa bado atakuwa ni wa baba yake maadam anafahamika baba yake kiusahihi pasi na mashaka” Shekh alizungumza kiufasaha kabisa.

“Kwamaana hiyo leo hakuna ndoa hapa?” mzee Mudy akahoji swali lile kwa umakini mkubwa.

“Swadakta! Itafaa kuwa hivyo. Jambo linalofaa vijana hawa kufanya kwa sababu wamemkosea Allah (Subhaanahu wa Ta'ala) kwa kuingia katika madhambi ni kurudi kwake na kumuomba msamaha, kuweka Niyah ya kutorudia tena kosa hilo na kufanya mema” alizungumza Shekh kwa kirefu na ufafanuazi mzuri ambao ulieleweka na kila mmoja katika kikao kile cha dharura.

*****

Sijui nizungumze nini kwa kila jambo ambalo nilikuwa nimekumbana nalo. Lakini niliweza kuvumilia katika kipindi chote hicho cha ujauzito na hatimaye kufanikiwa kujifungua mtoto wa kiume. Kama ambavyo nilikuwa nimeahidi ndivyo nilivyofanya kwa kumpatia jina mtoto wangu na kumuita Sekiza.

Kitu kikubwa ambacho hadi leo hii ninajivunia ni kwamba Fadhili aliendelea kunipenda na hata baada ya kujifungua tulifuata taratibu zote za kutubia dhambi ile tuliyokuwa tumeifanya mbele za Mwenyezi Mungu.

Kama ambavyo tulikuwa tumekubaliana siku ilipobatilishwa harusi kati yangu mimi na kaka Imran ndivyo tulivyotekeleza. Taratibu zote zilifuatwa baina ya pande mbili na hatimaye mimi na Fadhili tukafanikiwa kufunga ndoa na kuwa mke na mume halali.

Ninatoa shukrani zangu za dhati kwa shemeji yangu kipenzi Imran kwa kunipatia heshima kama shemeji yake na kusahau changamoto zote zilizokuwa zimejitokeza katika maisha yetu. Vile vile natoa shukurani zangu za dhati kwa wifi yangu Mainaya kwa kuishi na mimi kwa upendo na amani iliyojaa furaha utafikiri hatujawahi kukwaruzana hata kidogo katika maisha yetu. Mama na Baba Mkwe Bi Fatma na mume wake mzee Sekiza Mungu awapatie maisha marefu kwa kunipokea katika familia yao na kuishi na mimi kama binti yao wa kunizaa pamoja na kwamba changamoto kadha wakadha zilijitokeza.

Shukurani za pekee nazipeleka kwa wazazi wangu mzee Muhamedy pamoja na mama yangu mzazi Bi Zamda kwa kunilea katika maadili mema na kushikana na mimi katika changamoto za kimaisha ambazonilikumbana nazo.

Nitakuwa mchoyo wa fadhila kama nisipotoa shukurani zangu za dhati kwako wewe msomaji uliyefuatilia mkasa wa maisha yangu tokea msimu wa kwanza nilipokuwa kibinti kidogo hadi leo hii nimefika tamati nikiwa na jumla ya watoto watatu ambao tunaishi katika familia yenye furaha na amani maeneo ya Kijitonyama jijini Dar es salaam…..

Nakushauri usiache kufuatilia simulizi za mwandishi Kizaro Mwakoba kwa mafunzo na Burudani. Nasema Asante na Ubarikiwe sana.??


MWISHO!


0 comments:

Post a Comment

BLOG