Search This Blog

Sunday, April 18, 2021

RAHA YA DAFU UCHOKONOLEWE - 3

  


Chombezo : Raha Ya Dafu Uchokonolewe 

Sehemu Ya Tatu (3)


“Unamaanisha nini?”

“Yeye si alinipa kazi ya kumtongozea Farida. Mie nikamuuliza mwalimu kwani mimi sio mwanamke hadi anitume nikamuunganishe kwa mwanamke mwenzangu?” alieleza Sarah huku akibwibwishuka kwa nyodo.

“Kwahiyo ukaamua kujimilikisha mwenyewe?”

“Sasa ningefanyaje shoga. Nilijua hata kama ningemwambia Farida asingekubali. Mwenyewe si unajua anavyojifanya ana msimamo”

“Mnh hongera dada mimi nakuaminia wewe katika mambo fulani”

“Chezea mimi wewe. Hebu niache nipumzike bwana mana kazi niliyofanya ni nzito”

“Kazi ya kumfukuzisha Farida Shule au kuna nyingine?” Alihoji Anitha.

“Wewe unaiona ndogo hiyo? Samaki mmoja kwenye tenga akioza mtoe umtupe asije akasababisha wengine wakanuka bila sababu” Alizungumza sarah huku akichezesha miguu yake pale kitandani.

****

Mama alinisukuma kwa nguvu na kunifanya nidondoke. Nilijigeuza na kulala kifudi fudi huku nikilia kwa kwikwi. Mwanamke yule alifika pale nilipokuwa nimelala na kunikanyaga mgongoni kwa hasira. Nilihisi maumivu yakisambaa kutokea kwenye mgongo na kuenea maeneo ya mbavuni. Kifua kikabana na kunifanya nipaliwe na mate ambayo yalinisababisha nikohoe mfurulizo.

“Kila siku ninapokuwa namkanya wewe unanijia juu na kuniona namnyanyasa, sasa leo umeona madhara ya kumlea mtoto kama yai?” Mama lizungumza na Baba huku mguu wake ukiwa bado juu ya mgongo wangu.

“Mimi nafikiri kumpiga sio dawa ya kutibu ugonjwa” Alizungumza baba pasipo kumtazama mama Usoni.

“Kwahiyo unataka nimuache tuendelee kumfuga sio?” Mama alihoji kwa jazba akiamini baba alikuwa akinitetea kama ilivyokuwa kawaida yake. Hata mimi mwenyewe niliposikia maneno yale yakitoka kinywani mwa Baba nilifarijika moyoni na kuhisi malaika wa huruma alimtembelea Baba yangu kipenzi.

“Mimi nafikiri ungeachana naye tu” Baba aliendelea kuzungumza kwa sauti ya taratibu kama vile hakuwa amekasirika.

“We mwanaume utaniharibia mtoto! Haiwezekani afanye mambo ya kishenzi huko halafu nimfuge” Mama alizungumza kwa jazba na kuinama pale nilipokuwa nimelala. Alinikaba shingoni na kukigongesha kichwa chini kwanguvu!

“Mama nisamehe nimekomaaa!” Nililia tena kwa sauti kutokana na maumivu niliyoyapata kwa adhabu ile ya kupigishwa paji la uso chini. Ndugu msomaji usiombe yakukute yaliyokuwa yananikuta mimi muda ule.



Kelele zangu nilizokuwa napiga zilinisaidia kwa kiasi fulani kwani baba aliinuka kutoka kwenye kochi na kuja kumshika mke wake mikono iliyokuwa imenikaba.

“Acha usije ukajitafutia matatizo” Baba alizungumza huku akiibabadua mikono ya mke wake kutoka shingoni mwangu.

“Niwache nimkomeshe huyu mshenzi” Alizungumza mama kwa ukali.

Baba hakujali maneno yale na kufanikiwa kudhibiti juhudi za mwanamke yule aliyekuwa amedhamiria kunitoa roho yangu.

“Wacha bwana utamuua bure” Alisema Baba huku akimvuta mke wake nyuma.

“Wacha nimuue kwani ana umuhimu gani kwetu zaidi ya kutupotezea pesa na kututia aibu. Unafikiri hayo aliyoyafanya si ni aibu” Alizungumza mama kwa jazba huku akinikazia macho ya kutamani kunivaa tena.

Masikini ya Mungu nilikuwa nimejikunyata pale chini utafikiri kifaranga cha kuku kilichokuwa kimepoteza mama yake. Sikuwa na pakushika wala mtu ambaye alisimama upande wangu kunitetea. Kwani hata huyo Baba mwenyewe hakuwa na imani tena na mimi.

“Samaki akichina hata umtie vitunguu saumu Elfu moja na tangawizi gunia zima, hawezi kurudi katika hali yake ya kawaida” Baba alizungumza huku akimuachia mke wake na kwenda kuketi kwenye kochi ambako alikuwa ameketi awali.

“Kwahiyo unamaana ameshindikana?” Alihoji mama huku akiwa amesimama na mikono ameiweka kiunoni.

“Huyo ameshindikana mama achana naye. Mwache akafie mbele huko” alizunguma baba huku amejilaza kwenye kochi na mIkono yake ameilalia kichwa kwa nyuma.

“Mimi siwezi kushindwa na haka ‘Kakimba’! Si Kimba tu huyu tumemnya wenyewe, iweje leo atushinde?” mama alizungumza kwa msisitizo.

“Atakuumiza kichwa tu mke wangu, mwache aende akawatafute wazazi wake huko mbele ya safari” Alizungumza baba huku akitikisa mguu wake wa kulia.

“Sisi ni wazazi wake, tusipo mfunza sisi atafunzwa na nani?”

“Atafunzwa na ulimwengu!” Baba alijibu kwa ufupi.

“Hakuna cha ulimwengu hapa, lazima nimnyooshe mwenyewe” Alisema mama huku akielekea kwenye kochi lingine na kuketi.

Masikini ya mungu pale chini nilipokuwa nimejikunyata niliendelea kulia na kulowanisha uso wangu kwa machozi. Binadamu wale hawakuwa wanajua kama walichokuwa wananitendea hakikuwa kinanistahili kabisa. Nilitamani Mungu ashushe malaika wake aje awaeleze ukweli juu ya kile kilichokuwa kimetokea shuleni kwetu, lakini maombi yangu yakaishia kuwa kama ndoto za alinacha ambazo ni za kufikirika tu.

“Humu ndani mimi ndio baba, kwahiyo lazima nisikilizwe” Baba alizungumza kwa majigambo.

“Sawa wewe ni baba lakini kwa upuuzi huu siwezi kukubali kabisa” Mama alizungumza kwa msisitizo huku akipumua kwa hasira.

“Sasa nitakachokiamua hapa sitaki kupingwa na mtu yeyote”

“Eeh kwani si tumekuzoea humu ndani, Ninapokuwa nakaonya haka kashenzi wewe unakuja juu na kuniona mimi ni mkosaji. Leo hii amekuja na ushenzi zaidi bado unalea maradhi” Alizungumza mama kwa hasira huku akinitazama kwa uchu wa kunitandika.

“Naomba uniache mama Farida, usinichanganye” Baba alizungumza kwa tahadhari.

“Usiniite mama Farida, sina mtoto mshenzi kama huyu mimi” mama alizungumza maneno makali ambayo yaliuchoma sana moyo wangu na kunifanya nijihisi mpweke hapa ulimwenguni. Sikuwahi kutegemea kama siku moja mama angeweza kuzungumza maneno makali kama yale.

Baba alinigeukia na kunitazama kwa sekunde kadhaa pale chini nilipokuwa nimeketi kwa kujikunja.

“Unanitazama nini, angalia macho yake yale utafikiri paka shume!” Baba alinibeza na kunitolea msonyo.

“Huna lolote, unajifanya kumbeza huku unamtetea. Mtoto ndio umekwisha muharibu hivyo” mama alizungumza kwa kebehi kumwambia baba ambaye alikuwa akinisemesha mimi.

Baba aligeuza macho yake na kumtazama mke wake aliyekuwa amekaa kishari shari pale kwenye kochi.

“Hivi una nini wewe mwanamke?” Alihoji baba kwa jazba.

“Ni kweli umeniharibia mtoto wangu bwana!”

“Unajua kuwa hata wewe unaweza kuondoka humu ndani mwangu?” Baba alizungumza kwa hasira baada ya kuona mke wake alikuwa amevuka mipaka.

“Potelea mbali, nitaondoka ubakie na mwanao mpate kuleana vizuri” alizungumza mama kwa jazba.

Baba alitikisa kichwa na kusonya kidogo kwa kuona mke wake alikuwa ameshindikana. Alinigeukia tena mimi na kunitazama kwa makini.

“Chukua virago vyako uondoke hapa ndani kwangu” baba aliizungumza taratibu kama vile alikuwa amelazimishwa.

Nilishituka sana baada ya kusikia kauli ile kutoka kinywani mwa baba. Nikahisi pengine masikio yangu yalikuwa na matatizo hivyo yalinifanya nisikie tofauti na maneno yaliyotamkwa. Nikatoa macho kwa makini kumtazama Baba huku nikitaka arudie kauli yake.

“Usinitazame, nimekwambia ondoka nyumbani kwangu! Sikuhitaji” Baba alizungumza kwa msisitizo jambo lililonifanya niamini kile alichokuwa anakizungumza.

“Baba naombeni mnisamehe sitarudia tena” nikazungumza kwa hudhuni huku nikiumia ndani ya moyo wangu. Iliniumiza sana kwasababu kosa ambalo nilikuwa naadhibiwa nalo halikuwa la kweli. Lakini ningefanyaje wakati sikuwa na mtetezi yoyote pale ndani.

“Kelele! Sitaki kusikia ‘Alifu’ wala ‘Bee’ hapa. Naomba uondoke!” baba alizungumza kwa ukali huku akiwa amenitolea macho kwa msisitizo.

“Lakini baba nitakwenda wapi mimi?” nilihoji huku nikibubujikwa na machozi.

“Sijui, nenda ukamtafute bwana wako, wewe si mkubwa sasahivi ushajua kutomaswa nenda huko huko” Alizungumza baba kwa msisitizo.

Mama ambaye alikuwa akigombana na baba kwa kudai kuwa mzee yule alikuwa akinitetea mimi, alipigwa na butwaa na kubaki ameduwaa. Nayeye hakutegemea kama baba angeweza kufikia uamuzi wa aina ile.

“Hayo ndiyo uliyokuwa unayatafuta sasa umeyapata” Akazungumza Mama kwa sauti ya chini huku akiwa na wasiwasi ndani ya moyo wake.

ENDELEA….19

“Nisameheni mama sitarudia tena mimi” niakazungumza huku nikilia kwa uchungu.

“Kwani mimi ndio nimekutuma ufanye ufirauni wako huo?” mama alijifanya kuzungumza kwa ukali huku akihisi baba alikuwa ananitisha tu na maneno yale.

“We mama, naomba ukitoe hiki kiumbe mbele ya macho yangu sitaki kukiona” baba lizungumza kwa msisitizo huku akininyooshea kidole.

Mama alitulia kidogo baada ya kubaini kuwa maneno yale hayakuwa ya masihara kama ambavyo alikuwa amefikiria awali.

“Usinitumbulie macho!! Toa takataka yako ndani kwangu!” Baba alizungumza kwa ukali na asauti ya juu kiasi cha kumfanya mama ashituke pale kwenye kochi alipokuwa ameketi.

Na mimi mwenyewe nilijikuta nimeinuka na kukimbilia pembeni mbali na pale alipokuwa ameketi mzee yule. Bado nilikuwa nikilia kwa kwikwi nikiamini viumbe wale wawili wangeweza kunihurumia.

Mama alinitazama kwa sekunde kadhaa kisha akavuta pumzi ndefu na kuzitoa taratiibu. ‘Uchungu wa mtoto aujuae mzazi’ akaanza kuhisi hali ya huruma ndani ya nafsi yake. Pamoja na kwamba alikuwa na hasira sana lakini alipokuja kusikia maamuzi ya Baba ambaye yeye alihisi alikuwa akinitetea akajikuta akiishiwa na pozi na kuhisi tumbo likimsokota.

“Nikiinuka hapa mnajua mtapata shida nyite wawili” Alizungumza baba kwa sauti kavu iliyokuwa imepoteza hata tone moja la amani.

“lakini mume wangu…..” mama alitaka kunitetea lakini kabla hajazungumza kile alichokuwa anataka kukitoa baba alimkatisha juu kwa juu.

“Sharap!! Sitaki kusikia neno lolote, nimeshasema Farida aondoke nyumbani kwangu fulstop!” Alizungumza kwa msisitizo.

“Baba Farida, huyu ni mtoto wetu. Akikosea tunapaswa kumuonya tu na sio kufikia huko ulikofika wewe” Mama alizungumza kwa kusihi na sauti yake ikiwa chini tofauti na awali.

Baba alijiinua kutoka pale kwenye kochi na kuvuta hatua ndefu kuelekea pale nilipokuwa nimesimama. Alikuwa amebadilika na kuwa kama mnyama wa mwituni. Macho yake yalikuwa mekundu utafikiri alikuwa akipika kwa kuni ndani ya chumba kidogo kisicho na dirisha. Midomo yake ilikuwa ikimcheza kwa hasira utafikiri mgonjwa wa Malaria aliyekuwa anatetemeka kwa baridi ya homa.

Mwanaume yule alinishika shingoni na kunitikisa kwa nguvu jambo lililonifanya nijikunje kwa woga na maumivu.

“Mama nakufaaa!” Nilipaza sauti za woga.

Uchungu wa mwana aujuae mzazi. Mama alikuja haraka sana pale tulipokuwa nimebanwa na kuanza kuminyana na mikono ya Baba kuichomoa shingoni mwangu.

“Basi mume wangu amekoma muache” Mama alizungumza kwa kusihi.

Baba aliniachia kwa kunisukuma kwa nguvu, nilipepesuka na kwenda kudondokea kwenye meza ndogo iliyokuwepo sebleni pale. Nilijigonga kwenye mbavu lakini maumivu sikuwa nimeyahisi kwa muda ule kutokana na lile tifu lililokuwa likiendelea ndani mle.

“Mume wangu, huyu mtoto ameshajifunza mwache sasa” Alizungumza mama kwa ile sauti yake ya kusihi.

“Nimuache kitu gani, lazima atoke ndani mwangu” Alisema baba kwa jazba.

“Lakini mume wangu, utakapomfukuza utakuwa haujamsaidia kitu”

“Nimsaidie nini? Tulipomsaidia panatosha ngoja aende mtaani huko akapatiwe msaada na watu wengine” Alizungumza baba Kwa jazba.

“Yani kweli mume wangu unataka kumfukuza mtoto?” Alihoji mama kwa mshangao.

“Sio nataka kumfukuza. Bali ndio namfukuza hivi. Aondoke akatafute wazazi wake mbele ya safari” Baba alitoa maneno hayo pasipo na hata chembe ya huruma.

“Hapana mume wangu mimi sikubaliani na hilo” Mama alizungumza kwa msisitizo. Huwezi kuamini kama mwanamke yule ndiye yule ambaye alikuwa mstari wa mbele katika kunipa adhabu kwa kosa lile walilokuwa wamenihukumua bila kugundua ukweli wake.

Nilijaribu kumtazama Baba kwa macho ya huruma nikiamini pengine angenihurumia lakini mambo yakawa tofauti kabisa.

“Usinitumbulie macho mimi kama Fundi saa aliyepoteza nati, ondoka nyumbani kwangu!” Alizungumza baba kwa sauti kuu iliyonifanya nizidi kutetemeka kwa wasiwasi na woga.

“Baba naomba unisamehe sito rudia tena” Nilijaribu kujitetea kwa mara nyingine huku nikilia.

“Inaonekana hamnielewi na mnafikiri nafanya maigizo hapa, subirini sasa” Alizungumza baba na kuondoka kwa hatua ndefu kulelekea jikoni. Pale sebleni tukabaki mimi na mama.

“Unaona sasa, umalaya wako umekuponza” Mama alizungumza kwa sauti ya chini huku akiwa amenikodolea macho kwa msisitizo.

“Lakini mama kweli mimi sikufanya kosa hili nimesingiziwa tu” Nilimueleza mama kwa upole.

“Usingiziwe wewe umekuwa nani? Mbona wengine hawajasingiziwa?” Mama naye alizungumza maneno makali na kusahau kama alikuwa akinitetea nisifukuzwe na baba.

“Kweli mama naomba mniamini, mimi siwezi kufanya mambo kama hayo. Katika maisha yangu sikuwahi kukutana na mwanaume hata siku moja” Nilizungumza kwa machungu.

Mama alinitazama kwa sekunde kadhaa kisha akameza funda la mate. Kusema ukweli alikuwa amekasirishwa sana na taarifa zile nilizokuwa nimekwenda nazo nyumbani pale, lakini pia akiwa kama mzazi aliyenibeba tumboni mwake kwa miezi tisa na kunizaa kwa uchungu, hakuwa tayari kuona baba ananifukuza ndani pale kirahisi namna ile.

“Hivi unafikiri nitafanya nini ili Baba yako akuelewe, na wewe mwenyewe unamfahamu vizuri” alisema Mama kwa sauti ya uchungu wa mzazi kutokea ndani ya moyo wake.

“Nisaidie mama, nitakwenda wapi mimi hapa Dar sina hata ndugu mimi” nilizungumza huku nikipiga magoti kumuomba mama anisaidiea kuniombea msamaha kwa baba.

Kabla mama haja zungumza neno lolote nikiwa pale chini nimepiga magoti, baba alitokea jikoni huku ameshikilia panga mkononi.

“Nakwambia utatoka au nikutenganishe shingo yako na kiwiliwili?” Baba alizungumza kwa jazba huku akinifuata kwa kasi pale sebleni.




Ndugu msomaji usiombe yakukute, mtoto wa kike nilijikuta nimesimama na kutikmua mbio kama mshale kutoka nje. Chezea panga wewe!

Baba naye akaniunganishia nyuma na kunitimua na panga lake mkononi. Alipoona nimetoka nje aliingia ndani na kuchukua yale mabegi yangu niliyokuwa nimetoka nayo shuleni na kunirushia kule nje.

“Nenda ukafie mbele Malaya wewe!!” Baba alipaza sauti baada ya kunirushia mabegi yangu nje.

Sijui kama ungekuwa wewe msomaji wangu ungefanyaje, lakini mimi moyo wa kurudi ndani mle ulipotea kabisa. Hivyo nikajikuta nikiokota mabegi yangu huku nikilia na kuanza kuvuta hatua mojamoja kuondoka nyumbani pale.

Kusema ukweli sikuwa naelewa ni sehemu gani ambayo ningeweza kuelekea baada ya kutoka pale. Mjini kwenyewe kama nilivyokwambia awali sikuwa na ndugu hata mmoja ambaye nilikuwa namfahamu pamoja na kwamba niliwahi kusikia kuwa kulikuwa na shangazi yangu anaishi maeneo ya Mbagara Rangi tatu. Unafikiri ningeanzia wapi kumtafuta mtua ambaye hata namba zake za simu sikuwahi kuwa nazo. Sio hivyo tu bali hata kumtia machoni sikuwa nimewahi.

****

Baaada ya baba kumaliza zoezi lake la kunitimua nyumbani kwake, alirudi ndani na kumkuta mama ameketi kwenye kochi huku amefura kwa hasira.

Walitazamana kwa sekunde chache utafikiri majogoo waliokuwa wakitaka kupigana. Kila mmoja alionekana kujawa na hasira dhidi ya mwenzake. Nafikiri mama alikuwa na hasira zaidi ya baba, alivuta pumzi ndevu na kuziachia kwa mkupuo.

“Umemfukuza sasa umepata faida gani?” Mama alihoji kwa jazba.

“Amepata haki yake” Baba akajibu kwa mkato huku akivuta hatua kuelekea kwenye kochi lake kuketi.

“Tatizo wanaume hamjui uchungu wa mtoto na ndiyomaana mnafanya vitu vya kinyama kama hivyo” Alizungumza mama kwa hasira.

“Siwezi kuendelea kuishi na toto lililokosa maadili hapa nyumbani kwangu”

“Hayo maadili angeyapataje kama haukumpatia?”

“Hakuna bwana, mambo ya ujingaujinga mimi wala siyapendi”

“kwani siku zote nilipokuwa nikimuonya wewe si ndiye uliyekuwa unanijia juu na kujifanya unampenda saana, leo amepatwa na tatizo unajifanya kumgeuka” Alizungumza mama.

“We mwanamke hebu wacha kunipigia kelele” Baba alizungumza kwa sauti ya chini lakini iliyokuwa na msisitizo.

“Nisikupigie kelele kitu gani, mtu unakuwa na roho ya kinyama utafikiri kitu gani sijui” Mama alizungumza kwa hasira.

“Kwahiyo unataka kusemaje?”

“Kama ambavyo umemfukuza mtoto wangu, namimi pia naondoka” mama alizungumza.

“Nenda, kwani si mnafundishana mitabia ya ajabu na ndiyo maana mnateteana” “Unanona unavyonitusi, yani mimi nimfundishe mtoto kufanya ufuska?” Alihoji mama kwa jazba.

“Nyamaza bwana, usinitibue na wewe” Baba alizungumza na kuinuka kuelekea chumbani akimuacha Mama katika wakati mgumu pale sebleni.

*****

Nlikuwa kama vile nimechanganyikiwa mtoto wa kike baada ya kukumbana na mabalaa yale. Sikuelewa kabisa nilichokuwa nimekikosea hapa duniani kiasi cha kufikia kuadhibiwa kiasi kile.

Baada ya kuhangaika kwa muda mrefu kutafuta mahali pa kujihifadhi nikajikuta nimedondokea kwenye mikono ya Mama Sakina, mwanamke ambaye miaka hiyo alikuwa ni Mama Ntilie maarufu pale Makumbusho.

Mama Sakina alikuwa ni mwanamke wa makamo aliyekuwa na watoto wakike wawili ambao alikuwa akiishi nao kwenye nyumba ya kupanga maene ya palepale Makumbusho. Namshukuru Mungu kwasababu Sakina na Halima walinipokea na kuamua kuishi na mimi kama ndugu yao wa damu.

Siku zote za uhai wangu nitaendelea kumshukuru Mama Sakina kwa wema aliokuwa amenitendea katika maisha yangu. Ndio Naomba Mungu ampe maisha marefu zaidi na zaidi.

Siku moja mama Sakina Alikuwa akiumwa hivyo ilimuwia ngumu kwenda kuuza chakula na badala yake ilitulazimu mimi na Sakina kwenda mgahawani kuokoa shilingi mbili tatu.

Nakumbuka siku hiyo nilikuwa jikoni katikaule mgahawa wetu nikifuta vyombo kwa kitambaa kwaajili ya maandalizi ya kifungua kinywa kwa wateja wetu. Ghafla Sakina alikuja na kunishika kwenye bega kwa ngyuma.

“Farida”

“Abee..” Niligeuka na kumtazama ndugu yangu yule usoni kwa umakini mkubwa kutokana na namna aivyokuwa ameniita.

“Naomba dakika tano tu!” Alizungumza Sakina kwa sauti ya kunongo’na.

“Dakika tano za nini?” nikahoji kwa mshangao.

“Huyo kaka hapo nje ni shemeji yako, nimemtafuta kwa muda mrefu mno leo ndio ameingia laini” Sakina alizungumza kwa msisitizo.

“Mnh!” Nilijikuta nikiguna kwasababu nilikuwa bado sijamuelewa dada yangu yule alikuwa na maana gani.

“Nataka leo nimpe mzigo hadi asinisahau katika maisha yake yote” Alizungumza Sakina kwa msisitizo na kumeza funda la mate.

“Lakini Sakina sio…” Nilitaka kumtahadharisha kwa jambo lile alilokuwa anataka kulifanya lakini aliniziba mdomo kwa kiganja cha mkono wake.

“Ya Sakina mwachie Sakina mwenyewe” alizungumza Sakina kwa msisitizo huku akinifungulia mlango wa jikoni na kunipa ishara ya kwenda nje.




Niipumua kwa nguvu kisha pasipo kuzungumza neno lolote lile mtoto wa watu nilivuta hatua na kutoka jikoni mle kwa shingo upande.

“Naomba niitie huyo mkaka, halafu wakija wateja waambie tumesitisha huduma kwa muda” Sakina alipaza sauti kuniambia nilipokuwa nikitoka.

Nisikufiche ndugu msomaji, nilikuwa nimechukizwa sana na kitendo kile alichokuwa anataka kukifanya Sakina. Mbona mama akiwepo hafanyi upuuzi kama ule? Nikavimba kwa hasira.

Nilipotoka nje ya mgahawa nilimkuta kijana mmoja mrefu mweupe ambaye hakuwa mnene sana wala hakuwa mwembamba. Nilitazamana naye kwa sekunde kadhaa pasipo kumsemesha neno lolote lile.

“Wewe ni malaika au umeshusha kutoka mbinguni?” Kijana yule alinisemesha huku akionkana kujawa na mshangao baada ya kuniona.

“We unaonaje?” Nikahoji kwa jazba.

“Sijawahi kuona msichana mrembo kama wewe tangu nimezaliwa!” Kijana yule akazungumza kwa msisitizo.

Niliinua macho yangu na kumtazama kwa jazba huku mapigo ya moyo wangu yakidunda mfurulizo bila kupumzika. Niliachia msonyo mrefu kama mkulima anafukuza ndege kwenye shamba la mpunga.

“Naomba usinizoee. Nenda ndani huko unaitwa na mshenzi mwenzio” Nilizungumza kwa msisitizo huku sura yangu imekunjwa kama ngozi ya tembo.

“Hakika wewe mtoto umebarikiwa!” Akazungumza huku akiingia mgahawani.

“Kwenda zako!”

“Samahani mimi Naitwa Dullah, Daktari wa mapenzi”

“Kwahiyo?”

Kijana yule alibusu kiganja ha mkono wake na kunirushia busu lile kwa ishara huku akitabasamu na kuramba midomo yake kwa uchu.

“Kafie mbele huko!” Nilizungumza kwa hasira huku nikigeuza shingo yangu kuangalia pembeni na kuachia msonyo.

Kijana yule alivuta hatua kuingia mgahawani mle huku akinikata jicho kwa macho ya tamaa.

Nilivuta hatua na kurudi mgahawani huku Sakina na mwanaume wake wakiwa jikoni wakifanya yao. Nililaani sana kitendo kile alichokuwa anakifanya Sakina kwenye mgahawa wa mama.

Nikiwa nimefura kwa hasira, sura ya kijana yule ikajirudia kwenye ubongo wangu na kuhisi kama vile kuna sehemu nilikuwa nimewahi kumuona. Nikajituliza na kuvuta kumbukumbu zaidi na mwisho nikabaini ni kweli niliwahi kumuona sehemu.

Kijana yule ndio yule aliyekuwa akimliza Anitha siku ile kule bwenini. Alikuwa anafanana kabisa na yule tuliyemuona kwenye picha aliyotuonesha Anitha. Lakini kilichonifanya niwena uhakika ni jina lake. Kijana yule wa kwenye picha alikuwa anaitwa Dullah kama alivyokuwa yule wa Sakina.

“Maweee! Hiyooo fanyaaa kwa hiviiiii aaaaah!” Niligutushwa na sauti ya Sakina kutokea jikoni ikilalamika. Nikainua kichwa ili kuweza kusikiliza kwa makini.

“Tulia baby usitikisike hivi itakuumiza” Nikamsikia kijana yule akizungumza.

“Utaniachia hii mashine nibaki nayo itanisaidia kila nitakapoihitaji heti babe” Sauti ya Sakina ikazidi kulalamika na kuzungumza maneno ambayo sikuwa nimeyaelewa.

“Chukua tu mtoto mzuri, najua umeitamani kwa muda mrefu sana” Alizungumza yule kijana.

“Ulikuwa unaninyima kumbe ni tamu hivi?”

“Pandisha hapo kwenye hiyo meza!”

“Meza…meza…meza ya mama mboooovuuuu!” Sauti ya Sakina ilinifanya nizibe masikio ili nisiendelee kusikia upuuzi ule uliokuwa ukiendelea kule jikoni.

“Nitanunua nyingine mpenzi, weka nikuoneshe utamu wenye hamu!” Pamoja na kuziba masikio lakini bado sauti nzito ya yule kijana ilipenya kwenye masikio yangu.

Nikajiinua kutoka pale nilipokuwa nimeketi na kusimama kwa hasira huku nimekunja sura utafikiri nimesikia harufu ya kinyesi. Nilivuta hatua kwa lengo la kutoka nje kabisa ili kukwepa ile kero ya sauti zao za ajabu lakini nilipofika mlangoni nikasikia sauti ya kitu kikivunjika kwachaaa! Nikasita kutoka nje na kusikiliza kwa makini.

“Ayaaa tumevunja!” Sauti ya kiume ilisikika ikihamaki.

“Nipe bwana achana na meza, Oooooh baby kumbe hata kwa hivi ni tamu!” Sakina akazungumza kwa ile sauti yake ya kulalamika.

“Inamaana hauumii kwa staili hii?” Sauti ya kiume ilihoji.

“Sijui kama naumia lakini nasikia utamu, weka tu mwanaume wewe ndiye kidume baba” Nakwambia Sakina alizidi kulalamika utafikiri anachinjwa.

Nilijiona mpumbavu na mjinga mara dufu kwa kuruhusu jambo lile litokee. Nikapandwa na hasira na kugeuka kuelekea kwenye mlango wa jikoni ambako nilianza kugonga mlango kwa nguvu.

“Sakina hebu fungueni mlango” Niipaza sauti kwa jazba.

“Baba naku… Nako…naku…Nakufaaa!” Sakina aliendelea kulalamika kule jikoni na kubaini kuwa walikuwa hawanisikii kabisa kama nawagongea mlango.

Ghafla nilisikia sauti za vyombo vikiporomoka kutoka kabatini kama vile kabati limedondoshwa.

“Mungu wangu! Hawa washenzi watamaliza vyombo vya mama” Nikazungumza kwa wasiwasi huku kifua changu kikijaa hasira zaidi na zaidi.

Baada ya sauti za vyombo kimya kikatawala kwa sekunde kadhaa utafikiri wawili wale walikuwa wamekata roho mle jikoni. Nikapatwa na hofu zaidi na kuhisi pengine watu wa watu walikuwa wamegandamizwa na kabati la vombo.

“Nyie kunguni mpo hai au mmekufa?” Nilihoji huku nikitega sikio kusikiliza kwa makini sauti kutokea jikoni.



Mara mlango wa jikoni ukafunguliwa na kale kakijana kakachomoja utafikiri nyoka anatoka shimoni. Alikuwa amevaa tabasamu la aibu huku akicheka cheka.

“Aaah Mrembo naona upo beneti na nduguyo!” Kijana yule alizungumza kwa sauti ya hini ili Sakina asimsikie.

“Hebu changanya makongoro na upotee machoni mwangu!” Nilizungumza kwa sauti ya chini kama yake lakini iliyokuwa imejaa ghadhabu.

“Mimi ninaitwa Dulah, Daktari wa mapenzi!”

“Kwahiyo?”

“Dozi zangu huwa ni za uhakika, hazinaga mushkeli!” Kijana yule aliyejitambulisha kwa jina la Dulah alizungumza.

“Hebu potea kwenye macho yangu nisije nikatapika” nilizunguza huku nikivuta hatua kuingia jikoni na kumuacha Dokta Dulah akinikodolea macho.

Ni yeye kabisa aliyekuwa mpenzi wa Anitha. Nilipokuwa nazungumza naye nilijitahidi kumtazama kwa makini usoni na kuthibitisha kuwa ni yeye. Mshenzi mkubwa inaonekana ni mchafuzi wa mazingira.

Nilimkuta Sakina ameketi kwenye kiti huku akiwa amechoka utafikiri alikuwa akisukuma maloli mabovu ya kubeba mchanga. Vyombo vilikuwa vimesambaa kila sehemu na ile meza ya mama ilikuwa imevunjika utafikiri imepondwa kwa mawe.

“Pole kwa kazi. Naona mlikuwa mafundi selemala sijui mafundi wa nini maana jiko mmelisambaratisha” Nilizungumza kwa kebehi huku nikitazama jinsi waivyokuwa wamevuruga chumba kile ha jiko.

“Shoga we acha yule sio mwanaume bali ni mashine” alizungumza Sakina kwa majigambo.

“Hakika ni mashine maana amejua kusambaratisha jiko letu” Nikazungumza kwa kebehi.

“Yaani mwili wangu hapa utafikiri umevunjwa vunjwa, nipo hoji bin taaban” Sakina alizungumza huku akiegemea kwenye kiti.

“Lakini sio vizuri kabisa ulivyofanya Sakina”

“Hivi umeshawahi kushikika wewe au unasema tu”

“Kushikika na nini sasa?”

“Na hamu!”

“Hauna akili timamu wewe”

“Hata wewe siku ukibanwa mimi nitakupa nafasi ya kuhudumiwa” Sakina akazungumza kwa kujilazimisha huku akitazama pembeni.

Nilimtupia jicho la nyodo huku nikiendelea na shughuli za mgahawani ambazo zilikuwa zimetupeleka pale.

****

Kitendo kilichofanywa na Sakina kule mgahawani kilivuruga kabisa ubongo wangu kiasi cha kunifanya niwe kama vile nimepumbazwa akili. Usiku sikupata usingizi kabisa kutokana na mawazo yaliyoletwa na kujirudia kwa tukio lile.

“Farida …” Dada Halima aliita kwa sauti ya upole.

“Abee..”

“Haujalala?”

“Hapana dada nimelala” Nikajibu kwa ufupi.

“Aliyelala anazungumza?”

“Nilikuwa nimelala” Nikajibu.

“Naomba ulale kabisa na kama huwezi kulala basi toka nje” Alizungumza dada Halima kwa sauti ya upendo lakini iliyojaa msisitizo.

“Niende nje usiku huu jamani dada Halima?”

“Sasa kama hutaki kulala, kitandani unasubiri nini? Si uende nje ukafanye kazi ya ulinzi” Dada Halima alizungumza kwa sauti ya upole.

“Basi dada Halima ninalala” Nikajibu kwa sauti ya upole.

“Nyamaza bwana, unalala huku unazungumza! We vipi?” Akazungumza kwa ukali kidogo na kunifanya niingiwe na woga kidogo.

Ilinibidi ninyamaze na kujifunika shuka hadi usoni pasipo kuendelea kuzungumza tena. Nikajilazimisha kupata usingizi lakini bado mawazo ya yale yaliyotokea kule mgahawani yaliendelea kunitawala.

Ghafla nikasikia dirisha la chumbani kwetu likigongwa taratiibu. Nikaacha kupumua ili kuweza kusikiliza kwa makini. Nikweli kabisa dirisha liliendelea kugongwa ingawa kwa hatua za kusikilizia majibu. Nilijikuta nikipatwa na hofu huku mapigo ya moyo yakinienda mbio. Nikavuta shuka na kujifunika zaidi huku nikijikunyata na kufumba macho kwa nguvu.

Nikiwa nimejikunyata katika hali ile ya kuogofya, nilimsikia dada Halima akifungua komeo za mlango taratiibu. Nilitamani nimwambie asifanye kitendo kile cha hatari kwasabau hatukumfahamu mtu aliyekuwa anatugongea lakini woga ulinizidi na kujikunyata zaidi. Nilifunua shuka kidogo kuweza kumuona aliyokuwa akifungua mlango ule.

Mapigo ya moyo yalizidi kunienda mbio baada ya mlango ule kufunguliwa. Nilimshuhudia mwanaume akijitoma ndani na kusimama nyuma ya dada Halima.

“Mungu wangu leo tumekwisha!” Nikazungumza kimoyomoyo huku nikihisi kutetemeka kwa hofu na mashaka.



Nilikaza macho kupitia kwenye ule upenyo wa shuka niliokuwa nimeuwacha kidogo na kumshuhudia mwanaume ule akikamata kiuno cha dada Halima na kumvutia kwake.

Halima aligeuka ghafla na kumkumbatia mwanaume yule huku wakimimiana mabusu motomoto na ndimi zikisabahiana kwa shangwe na vigelegele.

Nilivuta pumzi na kuziachia kwa kuzisukuma nje kwa nguvu huku nikifumba macho yangu kwa matumaini kiasi. Nikameza funda la mate kisha nikatumbua macho yangu kuweza kushuhudia kile kilichokuwa kinataka kuendelea ndani mle.

“Vipi Sakina ameshalala?” Nilimsikia mwanaume yule akizungumza kwa sauti ndogo huku wakivutana kuelekea kwenye kitanda cha Halima.

“Sio Sakina, huyo ni yule mdogo wangu niliyekuelezaga” Halima akazungumza huku akifungua vifungo ya shati la mwanaume yule kwa spidi ya roketi ya kimarekani.

“Ahaa ndio kale karembo?”

“Acha basi habari zako, karembo umekaona wapi?” Halima akahoji huku akishika pua ya kijana yule na kuitikisa kidogo kimahaba.

“Nasikia sikuhizi mnauza sana mgahawani kwasababu ya huyo mrembo wenu”

“Acha basi Dullah, mimi ndio mrembo kuliko wote unaowafahamu wewe” Halima alizungumza kwa kujisifia huku akinitupia jicho kuona kama nilikuwa nimelala.

“Sakina amekwenda wapi?”

“Sakina amelala na mama leo”

“Sasa huyu dogo ataweza kuhimili vishindo kweli” Kiajana yule alizungmza huku akinitupia jicho na kumeza funda la mate baada ya kuona mzigo wangu umeinuka pamoja na kwamba nilikuwa nimeufunika kwa shuka.

Macho yangu yaliyokuwa yakichungulia katika kaupenyo yaliweza kusaidia kumuona vizui kijana yule usoni.

“Mungu wangu!” Nikajikuta nikihamaki baada ya kumtazama vizuri usoni.

Kijana yule alikuwa ni Dullah. Ndio ni yule Dullah aliyekuwa akifanya majambozi na Sakina kule mgahawani na kutuvurugia jiko letu. Ni yule Dullah aliyemliza Anitha kule shuleni na kumnyima amani katika masomo yake. Nikakaza macho ili kuweza kuthibitisha ukweli wa jambo lile.

Nilimshuhudia Dullah akidaka mguu wa kushoto wa Dada Halima na kuuweka juu ya kistuli huku mikono yake akiizunguusha nyuma ya kiuno na kupapasa madafu kwa mtindo wa kuyatomasa tomasa.

“Ishssss…..Aaaaa…Hapa ndio huwa unanimaliza Dullah wangu!” Alizungumza dada Halima huku akibenjuka kwa nyuma na kubinua kifua chake mbele kilichokuwa kimepambwa kwa matikiti yaliyotuna vyema utafikii vyungu vya kuchomea ubani.

“Mimi naitwa Dullah! Daktari wa Mapenzi” Kijana yule alizungumza huku mikono yake ikiyasabahi yale madafu yaliyomtembelea kwa dharula.

Maneno ya kijana yule yalinikumbusha kauli ya Dullah wa Sakina nilipokutana naye kule nje ya mgahawa. ‘Mimi naitwa Dullah, Daktari wa mapenzi’

“Inamaana Sakina na dada Halima wanachangia mwanaume mmoja?” Nikawaza kwa mshangao huku nikihisi moyo ukiniuma kwa hasira.

Dullah Alipeleka modomo yake na kupokea matikiti yale kutoka kwenye mikono yake halafu mkono mmjoa ukashuka chini na kupenya njiapanda na mkono wa pili ukarejea kwenye madafu ya kiunoni kuipa sapoti midomo yake iliyokuwa ikifyonza uatafikiri katoto kachanga.

“Aaaah! Dokta usifike huko!” Dada Sharifa alilalamika huku nikimshuhudia akishtuka na kupepesuka kutaka kudondoka.

Moyo ulipasuka Paaa! Nikiamini tayari dada yangu amedondoka lakini Dulah alimdaka na kumuinua kwa kumkamata kiunoni vyema. Nikaendelea kushuhudia dada Halima akibebwa juujuu kama kipane cha karatasi na kuwekwa kitandani na kijana Dullah.

“Mnh kuna watu wana nguvu” Nikajisemea baada ya kushuhudia kitendo kile.

“Dullah nipe matibau nime…nime…nimezidiwaaaah!” Masikini Halima alilalamika utafikiri amekabwa koo.

Kijana yule ambaye alikuwa bize tangu aingie chumani mle alimkamata kiunoni Halima na kumkunja kama chapati kisha aka jipinda kwa nyuma kidogo na kuinamia huku akiunguruma kama nguruwe.

“Mungu wangu! mauaji gani haya yanaenelea humu ndani?” Nikajikuta nikihamaki baada ya kushuhudia jinsi dada yangu alivyokuwa amekunjwa.

“Wayaaah! Kitu…kitu….kitu….Ooooh!”  Nilimsikia Halima akigugumia kwa kujikakamua kama vile amekandamizwa na kunia la mawe.

Niliogopa sana na kutamani kujiinua kutoka pale kitandani na kwenda kumsukumizia mbali mshenzi yule ambaye hakuwa na huruma kwa watoto wa wenzake.

Wakati Halima alipokuwa akijilalamisha pale kitandani, Dullah yeye alikuwa akikukuruka kwa kujizunguusha utafikiri feni huku akiwa amemtaiti kisawasawa dada yangu kipenzi masikini ya Mungu.

Nilivuta pumzi na kuziachia kwa nguvu kisha nikafumba macho kwa sekunde mbili tatu hivi kisha nikahesabu hadi tatu kwa lengo la kujiinua na kwenda kuokoa maisha ya mpendwa wangu Halima. Sikuwa tayari kuendelea kushuhudia mwanaume mshenzi akiutoa uhai wa kipenzi changu, tena kwa makusudi.



“Dullah hivyo hivyo…Nasikia raaaaha!…utaaamu!...Leo umenikuna vizuri Dullah wangu!” Mnh Halima akalalamika kwa kuzungumza maneno ambayo yalinifanya nisitishe shambulizi langu la kuvamia na kumuokoa.

“Eboo!” Nikahamaki kwa mshangao.

“Dullaha wangu mtamu kama sukari, wanoga kama asali….Nipe Dullaha nipe mume wangu kipenzi!” Halima aliomboleza.

“Mshenzi wewe utakufa huku unashangilia” Nilizungumza huku nikiahirisha zoezi la kwenda kutoa msaada. Sasa utamsaidiaje mtu ambaye mwenyewe anafurahia kukunjwa kunjwa na kufinyangwa kama tonge.

“Dullah ukinisaliti nakuua, sio kwa utamu huu unaonipa…Hayaaah nenda kwa hivi! Ewaaaah!” Alilalamika Halima.

“Mnh! Au kuna raha kweli anayoipata mbonda anafurahia?” Nikajiuliza huku nikiednelea kutoa macho.

Ghafla nilimshuhudia Halima akifyatuka kama mtego na kujirudisha nyuma kwa spidi ya ajabu huku ametoa jicho utafikiri samaki ametolewa ziwani na mdomo ameufunua utadhani anaimba kiitikio cha kwaya.

“Sasa mbona kama anakata roho!” Nikazungumza kwa kuhamaki huku nikihisi mapigo ya moyo wangu yakinienda mbio.

Nikiwa katika hali ya mshangao na maswali yaliyokosa majibu, dada Halima alijirusha na kupeleka mdomo wake kwenye shingo ya Dullah na kumng’ata kama vile anauma kipande cha mnofu wa nyama ya kuku.

Masikini ya Mungu Dullah wa watu alifurukuta kwa kutaka kujinasua kutoka kwenye mikono ya Halima mla nyama za watu lakini akabanwa zaidi utafikiri alikuwa amenaswa kwenye shoti ya umeme.

Baada ya sekunde kadhaa nilimshuhudia dada Halima akitapatapa kama vile anakata roho huku akimkumbatia zaidi Dullah ambaye kijasho kilikuwa kinamtiririka huku akigugumia utasema amefundia makaa ya moto mdomoni.

“Sasa mbona wanauana hawa watu Mungu wangu?” Nikajiuliza kwa mshangao huku nikihisi mwili wangu ukitetemeka kwa hofu na kijasho chembaaamba kikitiririka kwenye maungio ya mwili wangu.

Dada Halima alivuta pumzi na kuziachia kwa nguvu kwa kupitia mdomoni kisha akatulia kama vile tayari ameshaaga dunia. Dullah naye akajitupa pembeni na kulala chali utafikiri anasubiri kufanyiwa uparesheni ya ngiri.

“Inamaana dada Halima ndio amekufa kwa staili hii?” Nikajiuliza kwa mshangao huku nikijitahidi kuzuia pumzi isitoke kwa sauti kutokana na hofu iliyokuwa imenijaa.

Ghafla Dada Halima akakohoa mara tatu mfurulizo huku akijiinua na kujisogeza alipokuwa amelala Dullah.

“Babaa” Aliita Halima kwa sauti ya uchovu huku akijilaza kwenye kifua cha Dullah.

“Vipi baby uko poa?” Dullah alihoji kwa sauti nzito.

“Kwanini nisiwe poa wakati Daktari wangu upo”

“Vipi lakini umefurahia shoo?” Alizungumza Dullah huku akichezea nywele za dada Halima.

“Haujawahi kukosea Daktari wangu, kila siku ni zaidi ya jana”

“Unataka kuniambia nini?”

“Shoo ya leo ni moto wa kuotea mbali. Unaweza Dullah wangu, Tafadhali usije ukanisaliti na kumpa mtu mwingine utamu wangu” Dada Halima akazungmza kwa kulalamika huku wakitazamana na Dullah wake kwa ukaribu zaidi.

“Kwahiyo ndio ukaamua kuning’ata?” Dullah alizungumza huku akijishika shingoni sehemu ambayo ilitiwa meno.

“Mungu wangu nimekung’ata?” Halima akahoji kwa kuhamaki.

“Unajifanya hujui sio?”

“Hebu tuone, sijui kweli Babaa” Halima alizungumza kwa sauti ya kudeka huku akimtazama Dullah shingoni.

“Kuanzia leo nitakuwa navaa helment kujikinga na ajali kama hizi” Dullah akazungumza kwa utani.

“Bwana usiseme hivyo nitanuna, muone vile” Nakwambia mtoto wa kike akajidekeza.

Dullah alimshika Halima usoni na kumpiga busu kwenye paji la uso kisha akainuka na kuanza kujivalisha mavazi yake tayari kwa kuondoka. Halima alikuwa amejilaza akimkodolea macho mwanaume yule.

“Aah kidume changu hichooo!” Alijisemesha Halima huku akimtazama Dullah wake na kujiinua kutoka pale kitandani. Akachukua upande wa khanga na kujifunga kifuani kwaajili ya kumsindikiza.

“Sasa kesho mchumba” Dullah akazungumza huku akifunga kifungo cha suruali.

Halima alifungua mlango na kuchungulia nje kuona kama kulikuwa na mtu pale nje. Alipohakikisha kuwa kulikuwa salama akarejea chumbani na kumpa ishara ya kutoka.

“Kesho usichelewe sana basi” Halima alizungumza kwa sauti ya kumtoa nyoka pangoni.

“Nitawahi halafu olewako uning’ate tena” Shabanializungumza huku akichomoka chumbani mle kama panya anavyotoka kwenye shimo lake.

“Muone vile” Alizungumza Halima kumsindikizia Dullah wake kisha akafunga mlango na kurejea kitandani.

Ndugu msomaji nakwambia pale kitandani nilikuwa nimebaki mdomo wazi kwa yale mauzauza niliyokuwa nikiyashuhudia kwa macho yangu siku ile. Yani unaweza ukasema ni filamu la kihindi sijui la kikorea yani presha ilinipanda na kunishuka na mwisho nikaachwa mdomo wazi.

Nilihisi hali isiyo ya kawaida katika maeneo ya Kijitonyama. Ndio hali haikuwa ya kawaida kwasababu mawingu sikuyaona wala mvua ilipokuwa ikinyesha, cha ajabu ni kwamba mtaa mzima ulikuwa umetota chapaa! Wakubwa wamenielewa?? Watoto mkakojoe mkalale



Hata hivyo sikuendelea kuumiza kichwa changu juu ya hilo na kujifanya kama vile yalikuwa hayanihusu.

Nilikumbuka shughuli aliyokuwa ameifanya Dullah na Sakina kule mgahawani kiasi cha kufikia kuvunja meza na kupasua vyombo vya mama. Nilioanisha tukio lile na songombingo la usiku na kujikuta nikichoka kabisa.

“Sasa mbona mapenzi ni kama vita?” Nikawaza mwenyewe pale kitandani baada ya kupata dondoo mbili tatu za mchezo huo.

“Kwakweli mapenzi nimeyachukia!” Nilizungumza huku nikijigeuza na kugeukia ukutani na kuanza kuutafuta usinginzi kwa nguvu.

*****

Tabia na mienendo ya ndugu zangu wale wa kishuzi nilizichukia sana kiasi cha kujikuta nikitamani kuondoka nyumbani kwao. Akili yangu ilifanya kazi kwa nguvu sana lakini sikuweza kufahamu ni kwa namna gani ningeondoka na ningekwenda kuishi na nani ambaye angenipokea kama walivyonipokea wao.

“Mvumilivu hula mbivu” Nlijipa moyo na matumaini huku nikiinua ndoo iliyokuwa na mchuzi wa nyama kwaajili ya kuelekea mgahawani.

Hali ya mama ilikuwa bado haijatengemaa hivyo mimi na Sakina tulipaswa kuendelea na biashara ya mgahawani wenyewe. Hata hivyo shughuli zote za maandalizi ya chakula zilikuwa zikifanyika nyumbani.

Nakumbuka nilikuwa njiani kuelekea mgahawani huku kichwani nikiwa nimebebelea ndoo iliyokuwa imejaa wali na mkononi nimeningi’niza kindoo kidogo kilichokuwa na mchuzi wa nyama.

“Mrembooo” Nikasikia sauti ya kike ikiniita kutokea upande wa pili wa barabara.

Niligeuka taratiibu ili nisije kudondosha ndoo iliyokuwa kichwani na kumwaga chakula.

Macho yangu yaliweza kumuona Sarah yule binti niliyekuwa nikiishi naye chumba kimoja kule shuleni amesimama huku akiwa amejawa na tabasamu. Nilishangaa kumuona mazingira yale tena akiwa hajavaa sare za shule.

“We Sarah unafanya nini hapo muda wa shule huu?” Nikahoji kwa mshangao.

“Wakusoma nitakuwa mimi shoga?” Sarah akanijibu huku akivuka barabara na kunifuata pale nilipokuwa nimesimama mimi.

“Tena hata hujavaa sare za shule! Una hatari wewe”

“Shule ndio nini bwana weee! Mimi nimezaliwa kula raha na sio kuteseka na makaratasi”

“Mnh yani wewe bado hujaacha tu!”

“Shoga kama yalivyokushinda wewe na mimi hivyo hivyo, nimeshindwa kutumikia mabwana wawili” Alizungumza Sarah kwa kujiamini.

“We Sarah umeacha shule?”

“Kama wewe umeshindwa mimi ningewezaje?”

“Mungu wangu! Sarah hujafanya jambo sahihi?” Nikazungumza kwa uchungu mkubwa.

“Wala sio ajabu mimi kuacha shule. Ulianza wewe akafuata Anitha na baadae mimi mama lao” Alizungumza kwa nyodo binti yule.

“We Sarah unataka kusema Anitha pia ameacha shule?” Nikahoji kwa mshituko wa hali ya juu.

“Hajaacha bali amefukuzwa shule kama ulivyotimuliwa wewe”

“Mungu wangu! Amekosea wapi jamani” Nikazungumza kwa masikitiko.

“Mimba mama. Amechezea pampu akajaa”

“Anitha amepata ujauzito?” Nikazidi kushangazwa.

“Kinachonishangaza ni kwamba Siku alipotimuliwa amelia sana, kama ilivyokuwa kwako”

“Sasa kinachokushangaza ni kipi hapo”

“Mimi siwezi kulilia shule kama mjinga. Ndiomaana nimeacha shule na kuamua kuolewa”

“Masikini Anitha amepoteza bahati kama mimi” Nikazungumza kwa masikitiko ya hali ya juu.

“Aaaah tuwachane na hayo. Haya na wewe mandoo hayo asubuhi yote hii unayapeleka wapi?” Sarah akaniuliza huku akinitazama kwa macho ya kebehi.

“Napeleka chakula hapo mgahawani” Nikajibu kwa ufupi.

“Unauza mgahawa shoga?” Sarah akahoji kwa nyodo.

“Namshukuru Mungu kwa hili, mkono unafika kiywani kwa wakati”

“Haya mambo umeyataka mwenyewe Farida. Kama ungemkubali mwalimu James saa hizi angekuwa ameshakuoa” Sarah akazungumza kwa kebehi.

“Hebu tuwachane na hizo habari za kuolewa Sarah” Nikazungumza kwa msisitzio baada ya kuona anataka kuniletea habari za hovyo.

“Mtoto mzuri kama wewe unahangaika na mandoo mjini badala ya kutulia ndani na kutunzwa” Sarah alizungumza huku akijitingisha kwa ile nyodo yake.

“Una maneno wewe! Kwanini usiolewe wewe basi kama ni mazuri”

“He shoga unataka nikwambie mara ngapi? Hivi unavyoniona nimeshaolewa nipo kwangu na mume wangu tunaishi kwa raha mustarehe” Maneno ya Sarah yaliushitua moyo wangu kidogo na kuhisi kaubaridi kakipenya kwa kasi kwenye mishipa ya damu.

“Unashangaa? Utashangaa sana Mume wangu ndio huyo anakuja” Sarah alizungumza huku akinionesha mtu aliyekuwa akitokea kwenye mashine ya kutolea pesa sijui wanaita ATM.

Nugu msomaji nilipomtazama vizuri mwanaume yule sikuweza kuamini macho yangu, alikuwa ni Mwalimu James. Ni yule mshenzi aliyekuwa ameshirikiana na Sarah pamoja na Anita kunifukuzisha shule. Nikajikuta nikitetemeka mwili kwa hasira na ghadhabu.

“Babe unamkumbuka huyu?” Sarah alihoji wakati Mwalimu James alipotukaribia.

“Mnh Sura yake sio ngeni” Mwalimu James akajibu huku akijifanya kama vile amenisahau kabisa.

“Unakumbuka kale kasichana kalikofumaniwa bwenini kakifanya mapenzi na mlinzi?” Alisema Sarah kwa umakini.

“Ahaaa kwani ndio haka?”

“Nakwambia kamezeeka kama kamezaliwa mwaka 47” Alizungumza Sarah huku akiegemea kwenye bega la mwalimu James.

“Binti unachanganya mapenzi na shule?” Mwalimu James akahoji kwa kebehi.

“Unafikiri shule mchezo? Kusoma wito Baba” Sarah akajibu.

“Hata hivyo bado ni kazuri” Mwalimu James alizungumza huku akinitazama kuanzia chini hadi usoni.

“Unasemaje?” Sarah akahoji kwa kuhamaki baaa ya kumsikia Mwalimu James akinisifia.

“Nilikuwa nakwambia muangalie anavyosikia wivu bada ya kutuona pamoja” Mwalimu James akajibaraguza.

“Kwaherini wapendwa” Nikazungumza huku nikivuta hatu kuondoka na kuwaacha wakinikodolea macho.

“Dunia simama nishuke ya walimwengu yamenishinda” Nikajisemea huku nikiongeza mwendo kuwahi mgahawani.

“Mrembooo!” Nikasikia tena sauti ya mtu akiita kutokea upande wa kushoto jirani na barabarani.

Kwakuwa nilishazoea kusikia watu wakiniita mtaani hasa wanaume hivyo sikushituka na kuendelea na safari.

“Faridaaa!” Sauti ile ikaita jina langu na kunifanya nigeuze shingo kumuangalia mtu aliyekuwa akipayuka kulitaja jina langu mtaani. Laaahaula! Alikuwa ni Dullah. Ni yule Dullah Daktari wa mapenzi aliyekuwa anawatibia Sakina na Halima.

“Duh! kumbe ni hili Zombi!” Nikajisemea huku nikisimama na kumsubiria.




“Naomba nikusaidie mrembo wangu!” Dullah akazungumza kwa sauti ya unyenyekevu utafikiri kweli alikuwa ni mtu.

Nilimkabidhi ile ndoo ya mkononi kwasababu niliamini lilikuwa ni jukumu lake kwani ulikuwa ni mzigo wa vichenchede vyake.

“Hivi ni kwanini nimechelewa kukuona?” Dullaha akahoji kwa sauti ya chini huku akiramba midomoyake.

“Labda kwasababu nimechelewa kupita”

“Sio hivyo bwana mtoto mzuri”

“Sasa kama ingekuwa nimewahi na Sakina si ungewahi kuniona pia” Nikazungumza huku nikikumbuka ile shughuli yake ya jana alipokuwa na Sakina mchana halafu akakutana tena na dada Halima usiku.

“Ninamaanisha zamani ulikuwa wapi maana kama ningekuona wala nisingeshobokea vile vishankupe” Alizungumza Dulla huku akinitazama kwa jicho la kuibia.

“Vishankupe gani?”

“Si wale ndugu zako, watoto Malaya kama nini!” Alizungumza Dullah na kuufanya moyo wangu ushituke. Kumbe anawachanganya nugu zangu halafu anawaita Malaya? Pumbafuu, Sijui nimmwagie hii ndoo ya wali wa moto kichwani!

“Usitake kuniambia umevuruga wote wawili?” Nikahoji swali la mtego nikijifanya sifahamu kitu.

“Aaaah wapi, kwa bahati nzuri hakuna hata mmoja niliyempa utamu wangu” Dullah akajaribu kuongopa akifikiri simtambui shughuli yake.

“Na zile meza kule jikoni zimevunjwa na tetemeko la ardhi au panya?” Nikahoji swali la kishambenga kwasababu nilikuwa nafahamu mchezo mzima.

“Kumbe wewe unahisi nimekula ile kitu jana? Yani ile meza ilivunjika wakati Sakina alipokuwa anaminyana na mimi nimpe shughuli. Nilimsukuma kwa nguvu akadondokea meza na kuivunja” Dullah akajieleza mwenyewe akiamini ananiongopea.

“Kwahiyo unataka kuniambia haujawahi kutoka nao hata mmoja?” Nikazidi kudodosa.

“Farida unajua mimi sipendi maujinga ujinga! Tena yule Halima ndio aliniomba nimuoe kbisa lakini nikagoma” Dullah akazungumza kwa msisitizo mkubwa.

“Kwanini sasa umekataa kumuoa dadaangu?”

“Weeee! Si afadhali hata ningekuoa wewe mtoto mrembo na unajiheshimu”

“Eboo! Sasa utamuoaje shemeji yako?”

“Shemeji yangu kivipi?”

“Mwenyewe unajua”

“Lakini Farida mbona unakuwa mgumu kunielewa? Wale sijawahi kuwakubalia pamoja na kwamba wananitaka” Alizungumza kwa msisitizo mwanaume yule.

“Sasa kwanini uwakatae kwani sio wanawake?” Namimi nikahoji kwamsisitizo.

“Kwahio unataka kuniambia niwapitie wote wawili?”

“Ikiwezekana wapitie tu” Nikajibu kwa ufupi

“Siwezi kufanya huo uchafu mimi” Akajibu na kunifanya nihisi ghadhabu zikinipanda kwasababu ni kweli alikuwa anawachezea wapendwa wangu wote wawili halafu anajikosha kwangu.

“Kama ni hivyo basi chukua hata mmoja na umuoe” Nikazungumza kwa sauti ya upole.

“Thubutuuu! Kama kuoa ni lazima si afadhali nikuoe wewe”

“Umuoe nani?”

“Nikuoe wewe mtoto mwenye sifa za kuwa mke bora”

“Haya nashukuru kwa masifa uliyonipa” Nikajibu kwa ufupi baada ya kuhisi hali ya hatari kwa mkaka yule.

Tulipofika karibu na mlango wa mgahawani Dullah akanishika mkono kunizuia nisiendelee na safari kama vile kulikuwa na jambo la msingi sana alitaka kunieleza. Niligeuka na kumtazama huku nikimsikiliza kwa makini.

“Kwahiyo umekubali ombi langu?” Akahoji kwa msisitizo.

“Ombi gani?”

“La kukuoa wewe jamani mrembo”

“Eboo! Kumbe ndio ulikuwa unanitongoza hapa?” Nikahoji huku nimetoa macho kwa mshangao wa kebehi huku nikiangua kicheko.

“Jamani Farida sio kwamba nakutongoza bali najaribu kueleza hisia zangu” Alizungumza kwa kubembeleza kijana wa watu.

“Karagabaho na ubwezi wako! Sio kila mwanamke yupo kama unavyofikiria wewe” Nikazungumza kwa msisitizo huku nimemkazia macho.

“Lakini nakupenda Farida nifanye nini mama ili uelewe hisia zangu?” Mnh jamani mwenzenu nikazidi kujionea maajabu ya mwaajabu kuzaa mtoto kumuita Rajabu.

“Baba naomba ndoo yangu naona umeanza kuvuka mipaka!” Nikazungumza kwa hasira huku nikinyoosha mkono wangu kupokea.

“Hapana mrembo usiwe hivyo, nakupenda sana tafadhali pokea hisia zangu” Dullah akazungumza kwa kulalamika kiasi cha kunifanya nitamani kuangua kicheko kutokana na ule uongo wake.

“Sikiliza we kaka, naomba ujiheshimu na tena jiangalie sana” Nikazungumza kwa msisitizo mkubwa huku nimekunja sura na kumnyooshea kidole kwa onyo.

“Nyie kunguru wawili, huu ni muda wa kazi mapenzi baadae. Yaone kwanza hamna hata aibu!” Sauti ya Sakina ambaye alikuwa akitokea nyuma ya mgahawa kumwaga maji machafu ilitugutusha.

“Wooow Kina huyo! Nimekumisi mama” Dullah alipaza sauti na kuzungumza huku akijichekesha chekesha kama muuza karanga.

“Nyoo sura zimewakomaa utafikiri tofali za kuchoma!” Alizungumza Sakina kwa hasira huku akivuta hatu kukusogea pale tulipokuwa tumesimama mimi na Dllah.

“Kwani tumefanya kosa gani mpenzi?” Dullah alihoji.

“Nyamaza ngisi wewe! Unajifanya unampenda dada yangu kumbe unamzunguuka na haka kashetani” Nakwambia Sakina yakamtoka maneno machachu.

Nliipoona moto unawaka bila ya mafuta nikajiongeza na kutaka kuondoka kumuachia Dullah msala wake.

“Na wewe unakwenda wapi hebu rudisha mironjo yako hapa!” Sakina akanisemesha na kunifanya nisimame na ndoo yangu kichwani.

“Sakina umekuwaje leo?” Alihoji Dullah kwa jzba.

“Kelele wewe!” Sakina alijibu na kunigeukia mimi tukawa tunatazamana usoni kama majogoo. 



“Mbona sikuelewi Sakina?” Nikahoji kwa sauti ya upendo.

“Sasa kama hukunielewa naomba unielewe kuanzia sasahivi. Huyu anaitwa Dullah ni mchumba wa dada Halima” Alizungumza Sakina kwa umakini na msisitizio huku amenitolea macho.

“Lakini Sakina…” Dulah akataka kuzungumza huku akinitupia jicho kiwizi wizi.

“Lazima nije kumueleza Dada Halima kila kitu” Alisema Sakina kwa msisitzio.

“Usifanye hivyo Sakina, unajua ninampenda sana….” Alitaka kuzungumza kitu Dullah lakini akapata kigugumizi kumalizia kauli yake kwasababu alikuwa anajaribu kunidanganya kuwa hakuwa na uhusiano wa kimapenzi na wawili wale.

“Zungumza tu mbona unasita! Unampenda sana nani Mimi, Halima, au huyu simbirisi wako?” Sakina akahoji kwa ghadhabu na wivu huku ametoa macho kama samaki.

Maneno yale ya Sakina yalimjaza hasira Dullah na ghafla sana akajivuta na kumtandika kofi la kushitukiza hadi nikahisi maumivu utafikiri nilikuwa nimetandikwa mimi. Mwili ulinitetemeka na mapigo ya moyo yakazidi kwenda mbio kutokana na hofu ya kitendo kile.

Baada ya Dullah kufanya kitendo kile aligeuza na kuondoka akituacha mimi na Sakina tunatazamana kama majogoo.

Waswahili wanasema “Ikitokea mbabe amekuonea nawe tafuta mnyonge umuonee”. Sakina Alimeza funda la mate kwa shida huku macho yake yameiva kwa uchungu na hasira. Pasipo kuzungumza neno lolote alinisogelea na kuvuta mkono juu kwa lengo la kunitandika kofi kama lile alilokuwa amezawadiwa na Dullah wake.

Nilifumba macho kwa nguvu huku nikisikilizia kupokea kipigo kile kutoka kwa yule dada yangu wa kishuzi. Hata hivyo zilipita kama sekunde tatu hivi pasipo kuhisi maumivu ya mkono ule. Nilipofumbua macho nikaukuta mkono wa Sakina ukiwa hewani huku umekamatwa na mkono wa mtu mwingine. Nikamtazama mtu yule na kujikuta siamini macho yangu. Alikuwa ni yule babu mlinzi wa shuleni kwetu mzee Makwacha.

Babu mzee Makwacha alikuwa ameukamata vyema mkono ule huku akiwa amemtazama Sakina kwa hasira. Huyu ni yule mzee aliyenisaidia mara kadhaa kule shuleni nilipokuwa katika matatizo kama haya. Lakini pia mzee Makwacha ndiye mtu ambaye nilisingiziwa kuwa nina uhusiano nae wa kimapenzi na kupelekea kufukuzwa shule pamoja na nyumbani kwetu.

“Ni a che e e e !” Sakina alizungumza kwa jazba huku akiuvuta mkono wake kwa nguvu kutoka kwenye kiganja cha Babu Makwacha. Hata hivyo mzee yule hakumuachia na badala yake alimtikisa kwa nguvu kuashiria hasira.

“Babu muachie!” Nikajikuta nikiingilia kati na mzee yule akamuachia kweli kwa kuusukuma kwa nguvu mkono ule.

“Hata siku moja usije ukafikiria kumgusa huyu binti” Alizungumza mzee yule na kugeuka kuondoka pasipo kuongeza neno lolote lile.

Nilitamani kumuita mzee yule lakini nikajikuta nikipatwa na kigugumizi hadi alipokata kona na kutoweka kabisa katika mazingira yale.

“Ni nani yule?” Sakina akahoji kwa sauti ya umakini akihisi kulikuwa na kauhusiano kati yangu mimi na mzee Makwacha.

“Sifahamu…” Nikajibu kwa ufupi.

Sakina aligeuza macho yake na kuangalia ule upande ambao mzee Makwacha alielekea. Akameza mate kisha akaachia msonyo mrefu uliokuwa umejaa ghadhabu, hasira na chuki.

“Twende tukafanye kazi muda umeenda sana” Sakina alizungumza kwa sauti ya chini huku akiinua ndoo ya mchuzi na kuingia nayo mgahawani.

Namimi nilivuta pumzi ndefu na kuangalia kule alipokuwa ameelekea mzee Makwacha. Nilitamani sana kuzungumza naye lakini ningewezaje wakati alishaondoka kabisa. Hata hivyo nilifurahi sana kumuona babu wa watu akiwa huru uraiani kwasababu mara ya mwisho alikuwa amechukuliwa na wale Polisi wa kutuliza ghasia.

*****

Usiku wa siku hiyo ulikuwa ni usiku mgumu sana kwa upande wangu. Mambo mengi yaliyokuwa yamepita yalijirudia kwenye kichwa changu. Nilikumbuka jinsi nilivyokutana na Sarah pamoja na yule mshenzi Mwalimu James ambae alikuwa amezoea kuharibu maisha ya wasichana hasa wanafunzi wa shule. Kama haitoshi nilikumbuka namna ambavyo Dullah alipokuwa akinitongoza na kusababisha mwanaume huyo kugombana na Sakina.Tukio hilo lilipelekea macho yangu kumshuhudia mzee Makwacha akinisaidia kutopka kwenye kipigo cha Sakina halafu pasipo kuzunguza na mimi akatoweka. Lakini pia nilikumbuka jinsi dada Halima alivyomuingiza Dullah chumbani na kufanya yao huku nikishuhudia jambo lililonifanya nihamie chumba cha pili ambako nililala na Sakina na kumuachia Halima lichumba lake pekeyake.

“Farida..” Sakina aliita na kunigutusha kutoka kwenye mawazo.

“Abeee!”

“Mbona hulali?” Sakina aliuliza swali ambalo niliulizwa na dada Halima usiku uliopita na mwisho akaingiza Dullah chumbani.

“Mungu wangu! Inamaana Sakina naye anafanya mchezo kama ule ule?” Nikajiuliza kimoyomoyo pasipo kumjibu kitu.

“Si nakuuliza Farida mbona hunijibu?” Sakina akahoji kwa msisitizo.

“Sina usingizi mpendwa”

“Afadhali tu ulale maana sijui kama utaweza kuvumilia” Alizungumza Sakina kwa msisitizo mkubwa na kunifanya niingiwe na hofu zaidi.

“Kuvumilia nini tena?”

“Mimi nakushauri ulale, maana binafsi siyawezi” Akazungumza Sakina kwa tahadhari. 


ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

BLOG