Search This Blog

Tuesday, April 13, 2021

KIFO CHA MENDE - 3

  


Chombezo : Kifo Cha Mende 

Sehemu Ya Tatu (3)




     *ENDELEA NAYO...*

Mlinzi geti, akamwambia Husna... "Ndio maana mnatapeliwa katika mapenzi tu". Husna akamshikia kiuno mlinzi na akamwambia "Eeeh...!! Tuache tutapeliwe, wewe yakuhusu nini?". 

Mlinzi geti, hakuwa na jibu. Na wala hakutaka kushindana na Husna, kwani mwisho inaweza leta uhasama ndani ya nyumba. Na kutimuliwa mimi yeye akabakia, ndio mlinzi geti akaamua kuwa kimya kwani dawa ya mropokani ni ukimya tu. 

Husna aliingia ndani, na kuchukua simu yake kumpigia mam Halima. Kabla dakika mbili kupotea simu ya Halima ikiwa inaita akapokea.. 

Husna akijikelia kwenye sofa huku akiiweka simu katika sikio la kulia na kumsalimia... "Hellow mam Halima, uko wapi sahizi". 

Halima alishtuka pindi alipoulizwa uko wapi akiwa bado yupo kwa Hemedi, Halima akatamka kwa kudanganya tu. "Nipo hapa kwa mashoga zangu, nakuja sasa hivi"

Husna akamwambia, "Usichelewe sasa" Mam Halima akamjibu, "Kwani vipi mzee amekuja?" Halima aliuliza swali kwa Husna, maana alijawa na wasiwasi kama muasi. 

Husna akamjibu.. "Hapana bado hajaingia". Halima, akakata mawasiliano na Husna. Iliingia saa kumi na mbili jua likielekea kuzama, kwa gafla ya taharuki kuu honi ya gari ikasikika katika geti. 

Mlinzi hakuzubaa, akafungua geti kwa haraka sana. Husna akakurupuka katika dirisha na kuanza kuchungulia kutazama kwa kina gari hilo lilikuwa nila mzee Rajabu huku Halima bado hajafika nyumbani. Husna alishika kichwa na kujua leo hapata kalika katika nyumba. 

Mzee Rajabu, akashuka ndani ya gari lakini hakuwa na haraka ya kuingia ndani ya nyumba. Kumbe alikuwa amempatia kazi mlinzi yakumchunguza mke wake Halima. Bwana Rajabu akamuuliza mlinzi geti kumhusu mke wake. 

Mzee Rajabu akishika miwani na kumuuliza.. "Kijana nipe habari kabla sijaingia ndani". 

Mlinzi geti akitamka kwa wasiwasi.. "Boss, kwahakika bado hajaingia na ametoka tokea saa nne ya asubuhi na kuniambia, anakwenda kwa mashoga zake lakini mpaka sahizi hajarudi". Baada ya kumwambia bwana Rajabu maneno hayo, Mzee Rajabu akashtuka gafla, na hasira kumvaa mwilini mwake. Kisha akaingia ndani bila ya kumwambia chochote mlinzi. 

Kufika ndani, akamkuta Husna akiwa amekaa sebuleni huku akitazama Tv. Husna akahamaki na kumsalimia. 

Husna akajinyanyua na kumsalimia.. "Shikamoo mjomba?" 

Bwana Rajab, akamjibu "Marahabaa hujambo?" 

Husna akamjibu huku akijiweka sawa kanga yake.. "Sijambo mjomba, karibu sana. Na pole kwa uchovu". 

Bwana Rajabu, akajibu huku akijipumzisha "Nishapoa mjomba". Husna akamuuliza bwana Rajabu.. "Mjomba nikuletee kinywaji gani?. Bwana Rajabu, akamjibu "Niletee maji tu". Husna akaenda kumchukulia maji mzee Rajabu. Huku akitikisa kalio lake kwa mtetemeko wa lawama. 

Bwana Rajabu, akavutwa na fikra chafu huku akianza kumuwazia Husna... "Daah..!! Mtoto huyu, yani ananipa mshawasha wa ajabu sana kwa umbo lake lakuvutia".. 

Husna, akamletea maji mjomba na kumuwekea katika meza na kumwambia "Mjomba karibu maji ya kunywa". Mzee Rajabu, akamjibu "Asante sana mjomba"

Kabla ya muda haujapotea, honi ya gari nayo ikasikika nje ya geti. Mlinzi geti hakuchelewa kwa kazi yake akafungua geti, Halima ndio anaingia sahizi. Kabla hajafika ndani akakuta gari la mzee Rajabu likiwa limepakiwa, Halima alipatwa na mshtuko na mwili wote ukanyong'onyea kama kifaranga cha kuku. Halima akashuka ndani ya gari huku hajui atamjibu nini mume wake, kufika akamkuka mume wake akiwa amekaa sebuleni pamoja na Husna. 

Akasalimia huku akipita haraka haraka... "Assalam Alykum? " Akajibiwa kama kawaida ya salamu" kisha bwana Rajabu, akamuita Halima. "Mke wangu niambie umetoka wapi sahizi, kuanzia saa nne asubuhi mpaka sahizi saa kumi na mbili inaelekea saa moja? "

Halima, akitetemeka kisirisiri kwa hamaki kuu na kujibu "Nilikuwa kwa mashoga zangu mume wangu". 

Mzee Rajabu kwa kuwa ni mtu mwenye hekima na akili nyingi, akamuuliza tena "Unauhakika umetoka kwa mashoga zako?" 

Halima akamjibu "Ndio mume wangu." 

Bwana Rajabu, hakuamini hilo kwani alihisi ni uongo mtupu akamwambia kwa kumuuliza.. "Huko kwa mashoga zako, kulikuwa na tukio gani?. Halima akamjibu kwa kumpanga Bwana Rajabu. "Kulikuwa na harusi ya rafiki yangu sasa sikuwa na budi kwenda kumtembelea". Bwana Rajabu akamuuliza tena. 

Bwana Rajabu akiwa bado amekaa katika sofa lake akimuuliza mke wake Halima.. "Na kwanini hukunipigia simu ukanijulisha kwamba unatoka?" 

Halima, akamjibu mume wake kwa kuzidi kumpanga lakini aliupuuzia msemo unaosema kuwa "Njia mtu muongo ni fupi". Akamjibu "Simu haikuwa na charge mume wangu ilizima"

Bwana Rajabu akamuuliza tena taratibu "Na sahizi iko wapi simu yako?" Halima akamtolea simu na kumwambia "Simu nipo nayo hii hapa mume wangu"

Bwana Rajabu, akamwambia tena mke wake. Huku Husna akiona kama movie vile jinsi maneno yanavyopangwa kwa akili ya hapo kwa hapo. 

Bwana Rajabu akamwambia.. "Kama upo nayo simu, mpigie huyo rafiki yako mmoja nimuulize"... 



Bwana Rajabu, hakuamini kwa hilo akanyanyuka sehemu aliyokaa. Kisha akamsogelea karibu ya mke wake Halima, akamtazama machoni kwa dakika tatu. 

Halima hakuweza kuvumilia kwa jinsi anavyotazamwa kwa macho. Akakwepesha macho yake huku na kule, bwana Rajabu kwa vile ni mtu mwenye hekima akamwambia. "Mke wangu, ulitafutalo utalipata endelea...." Bwana Rajabu, akarudi sehemu yake aliyokuwa amekaa huku Husna akijiweka sawa kwa mikao ya mitego. 

Muda uliyoyoma na kila mmoja kwenda kulala, ilifika asubuhi wakati huo Husna ndiye wa kwanza kuamka na kuandaa kiamsha kinywa na vitafunio vya bwana Rajabu. Hili lilimfurahisha sana bwana Rajabu, kwa bidii alizokuwa nazo Husna. Na kuna wakati Halima akiwa amekasirika na kuchukia kwa kuhisi anaweza kupokonywa mume wake kwa bidii za Husna. 

Lakini Husna hakuwa na wazo hilo kichwani mwake, baada ya kumuandalia chai bwana Rajabu.  Husna alitoka nje ili kupunga upepo uliokuwa ukivuma, Halima akiwa bado amelala. 

Kwa upande mwengine, Mo Jay akiwa bado anahitaji penzi la Husna. Na kujaribu kumpigia ikawa simu haipo hewani. Alichoamua ni kwenda hadi kwao kuhakikisha yupo au la! Mo Jay alifika mpaka getini na kugonga geti hilo. Mlinzi akafungua geti ndogo na kumkuta Mo Jay nje ya geti mlinzi huyo akaamua kumuuliza kwa ukali swali hili "Kijana unataka nini usaidiwe?" Mo jay akamwambia kwa kukwepesha mada aliyokuwa nayo kichwani "Natafuta kazi yoyote ile, kama ipo niweze kuifanya". 

Mlinzi geti, akamwambia "Hebu ingia ndani, ukutane na boss mwenyewe". Mo Jay baada ya kuingia alianza kustaajabu ya musa badala ya firauni, kwa jinsi mandhari inavyopendeza magari yakiwa yamepakiwa nje. Kabla ya kupepesa macho bwana Rajabu akatoka nje kuelekea katika gari lake ili awahi kazini akatupia jicho kulia, akamuona Mo Jay lakini hakushughulika wala kumjua hapo mlinzi akamuwania katika gari na kumueleza. 

Mlinzi.... "Boss, samahani kwa usumbufu. 

Bwana Rajabu... "Bila samahani, niambie shida yako". 

Mlinzi akiweka sawa sauti na kumwambia.. "Kuna yule kijana anahitaji kazi yoyote ile humu ndani, lakini nikamwambia mpaka akuone wewe". 

Bwana Rajabu, akamjibu huku akiweka miwani yake sawa. "Mwambie apitie kesho Jumapili asubuhi,  na usimuache abakie hapa". Baada ya kauli kutemwa kwa bwana Rajabu, akawasha gari lake kwa kumuweka tayari kuchomoka. 

Mlinzi akamgeukia Mo Jay na kumwambia "Boss amesema, kwa leo haiwezekani njoo kesho Jumapili asubuhi". Mlinzi akafungua geti ili boss apite na gari lake. 

Mo jay, alitaka amuone Husna tu moyo wake utulie kwani walipoteana kwa siku kadhaa. Mo Jay, alirudi akiwa amepotelewa na furaha na huzuni kumuandama. 

Kulikucha kwa makucha yake asubuhi kufika , Mo Jay hakusahau vile alivyoambiwa. Kwani riziki huja kwa njia tofauti. Siku ya pili yake akaamua kwenda tena wala hakuchoka, kufika akafunguliwa geti kama kawaida yake. 

Akakutana na mlinzi geti. 

Mlinzi... "Ooh..!! Kijana umekuja tena, kweli uko na bidii ya kutafuta kazi. Mlinzi akamsifia kwa dakika chache. Huku Mo Jay akitabasamu na kumjibu. 

"Ndio nimekuja tena kwa mara ya pili". Lakini alitaka kitu kimoja kutoka kwa Husna. Lakini kilichomshangaza Mo Jay, hakuona dalili yoyote ya kuwepo kwa Husna. Alitaka kuuliza lakini alijikanya mdomo. 

Mlinzi akaamua kwenda ndani kumuita boss wake. "Boss samahani, kuna kijana amekuja anakuhitaji ". 

Bwana Rajabu akamjibu. "Mwambie aingie ndani". 

Mlinzi akarudi na kumwambia. "Ingia ndani kijana". Mo Jay, bila ya kupoteza muda, akafika mlangoni na kutamka "Hodii naomba kuingia" bwana Rajabu akamjibu "Ingia ndani" Mo Jay akaingia ndani na kumkuta Bwana Rajabu akiwa amekaa sebuleni pekeyake. 

Mo Jay, akamsalimia. "Shkamoo" 

Bwana Rajabu, akamjibu "Marahabaa karibu ukae unielezee". Kabla ya kuanza kujieleza Mo Jay akaitisha maji, ili ajue nani atakayemletea maji hayo.  "Kwanza naomba maji"

Bwana Rajabu, akaitisha maji.. "Husna lete maji mara moja". Bila ya kuchelewsha, Husna akaleta maji katika jagi kwa gafla wakaonana macho kwa macho na Mo Jay. 

Mpaka bwana Rajabu, akashtukia na kumuuliza Husna. "Vipi unamfahamu huyu..?"




Husna aliulizwa swali na Bwana Rajabu huku mwili ukimtutuma. Na akaamua kumjibu kwa jakajaka. "Ndio namfahamu mjomba" 

Bwana Rajabu, akamuuliza tena Husna. "Mwajuana kivipi kwa mfano?". Swali juu ya swali huku Mo Jay akaona kama nuksi vile kwake yeye na wala hakujua kama yatatokea haya. Husna akamjibu kwa sauti ya taratibu "Namfahamu zamani sana tulipokuwa shule ya msingi kisha darasa moja mjomba". Bwana Rajabu, akaamua kumwambia "Sawa unaweza kufuata shughuli zako unazotaka kufanya". Baada ya kuondoka kwa Husna, bwana Rajabu akamwambia Mo Jay. "Sema kijana tatizo lako ni nini?. 

Mo Jay, akikaa vizuri na kumueleza. "Mzee, mimi ni kijana ambaye natafuta kazi yoyote halali. Ili na mimi nipate riziki na nimezunguka kote na jua kali ndio nikaamua kuingia humu nistirike na mimi kwani vijana wengi ni wenye kasumba, naomba unisaidie mzee". Mo Jay aliomba kazi kwa Bw-Rajabu. Huku Husna akichungulia kwa kusikiliza, maneno na kuanza kujiuliza, "Kwani Mo Jay, anataka kazi humu ndani jamani". Bwa-Rajabu akamwambia. "Kijana nimekuelewa vizuri sana, ilikuwa tutafute mtu lakini umejileta gafla kama upepo. Sawa.."

Bw-Rajabu akaamua kumuuliza swali "Je unaweza kuendesha gari?" 

Mo Jay, akamjibu "Ndio naweza boss". 

Bwana Rajabu akamwambia. "Sawa kesho asubuhi uje na driving license, unipeleke kazini." 

Mo Jay, alifurahi sana moyoni mwake na kujua wazi kwamba mchezo ashafaulu. 

Baada ya siku nyengine kuwadia kama kawaida yake. Mo Jay, alijiandaa mapema na kufika kwa Bwana Rajabu huku akiwa amevalia suti lake jeusi. 

Alifunguliwa geti mara moja, akaingia ndani. 

Mo Jay akamsalimia mlinzi. "Za asubuhi mlinzi". 

Mlinzi akijibu. "Safi kaka karibu sana". Mo Jay, aliingia ndani zaidi kwa hatma akakutana na Halima mke wake Bwana Rajabu. Mo Jay, alishtuka kwa mara yake ya kwanza kuonana na Halima. Kwani aliona uzuri wa Halima jinsi toto lilivyoumbika kwa umbo takatifu. Mo Jay, hakujali akamtupia salamu. "Za asubuhi mamy?". 

Halima kwa upande wake, aliona kama ugeni. Na kumjibu "Safi, karibu ndani". Kabla ya hatua mbili kuisha, bwana Rajabu akatokeza akiwa amejiandaa vyema kabisa. Na kumwambia mke wake Halima, "Mke wangu, huyu ni mgeni wangu ndiye atakaye niendesha katika gari langu kuelekea kazini". Halima alimtazama Mo Jay kwa aibu ya macho huku akiwa anatamka. "Ni jambo zuri mume wangu heri ya kupumzika mikono yako. Na mimi pia atakuwa ananipeleka nikielekea shambani". 

Kabla ya muda kutaka kuyoyoma, bwana-Rajabu akampatia ufunguo Mo Jay. Kisha wakatoka nje, na kumwambia. "Nakupa ufunguo uanze interview." Mo Jay, hakuteteleka bali aliupokea ufunguo huo wa gari. Huku akishangaa na gari hilo la aina ya Range rover sport, ndio mara ya kwanza kuendesha gari hilo. 

Waliingia garini, kwa pamoja. Mo Jay, akawasha gari na likamkubalia kwamba limeshikwa na mtu mwengine. Mo Jay, alijiona mwepesi mithili ya pamba na geti likafunguliwa huku Mo Jay akilikonesha vyema kabisa gari hilo. Alimuacha Bwana Rajabu kinywa wazi kwani yeye hakuwahi kufanya hivyo, kisha kutoka nalo getini gari hilo kuelekea barabarani. 

Mo Jay, alijihisi kama yupo juu ya ndege jinsi gari anavyolitimua kisha akamuuliza bwana Rajabu. "Boss sahizi ni saa ngapi, nataka nifike kwa dakika kumi". Boss alimshangaa Mo Jay kwa kauli yake, kisha akamwambia "Sasa ni saa mbili kamili na natakiwa nifike na nusu". 

Mo Jay, kusikia hivyo alizidisha spidi mithili ya risasi huku bwana Rajabu akifurahishwa na kijana Mo Jay kwa utundu. 

Akaamua kumuuliza, "Kijana ulifunzwa wapi uendeshaji huu maana ndani ya dakika tatu tushavuka daraja la pili" Mo Jay akamjibu "Boss huwezi kuwa mzoefu wa kitu kama hujakizoea na kukiaminisha".. 

Ndani ya dakika kumi, Bwana-Rajabu kufikishwa kazini. Huku wajida wake wakimshangaa baada ya kushuka garini, na kuanza kumuuliza. "Boss leo umeamua mapema sana hata na nusu bado", 

Bwana Rajabu, akawaambia "Nimepata dereva hatari leo" kabla hajamaliza Mo Jay akatoka ndani ya gari ili wamuone. 

Kisha bwana Rajabu akamwambia Mo Jay, "Sasa unaweza kurudi nalo nyumbani kwangu kisha uje unichukue baada ya masaa manne yani saa sita uwe hapa". 

Mo Jay, akamjibu "Sawa boss"... Kisha akapanda ndani ya gari, bila ya kuchelewa. 

Mo Jay, alifika kwa haraka sana nyumbani kwa boss na kufunguliwa geti. Akaingia nalo ndani, kisha akaingia ndani zaidi baada ya kushuka garini huku Husna akihisi ni Bwana Rajabu kumbe ni Mo Jay. 

Akamkuta Husna ndiye yupo pekeyake katika nyumba hiyo akiwa amekaa, Husna akamwambia Mo Jay. 

Husna... "Karibu upumzike Mo Jay, na ajabu ni kwamba unaweza kuendesha gari kumbe."

Mo Jay akamwambia. "Kawaida, na hii funguo ya boss ya gari yake nataka kuiweka". Husna akaakamwambia "Njoo nikuonyeshe inapowekwa funguo hiyo" Wakati Husna yupo mbele ya Mo Jay, Husna alifanya kusudi kwa kutikisa makalio yake huku akiwa amevalia nguo laini na yenye kumtoa vyema umbo lake. 

Mo Jay, aliingiwa na jini mahaba bila ya kuchelewa akamshika makalio Husna. Husna alishtuka kwa mguso aliyoshikwa makalioni na Mo Jay, Husna alimpeleka Mo Jay katika chumba kinachowekwa huo ufunguo wa gari. 

Alipoweka ufunguo, Husna akamzuia mkono Mo Jay kisha akamwambia "Mo Jay nakumiss kwelikweli".  Husna akatupia mkono wake mbele ya suruali ya Mo Jay... 



Husna hakuona aibu wala utahayari kwani huu mchezo umekuwa mazoea kwake. Alizidi kutembeza mkono wake laini katika kifua cha Mo Jay, huku Mo Jay, akiwa tuli mithili ya maji mchunguni. 

Husna ni msichana aliyejaaliwa uzuri unaofuatia na umbo lake sawia lililoshiba vyema. Ama kweli wakubwa hufaidi vilivyo vizuri tu, Mo Jay kuona mchezo unaanza kunoga kwa Husna na yeye hakuachwa nyuma alimshika kiuno husna kiuno mithili ya kinu. 

Kushikwa tu, mtoto kujiachia kwa ulegevu na sauti kuitoa ya taratibu kama mtoto. "Aaaaaaaaaaah...mmmmmmnhhhh....aaaaaaiiiiissssshhhh.... endelea Mo Jay kunipapasa. 

Kwa kauli na msemo ulimfanya Mo jay kuzidi kumnogesha mwana wa watu, Husna kuona mambo yashakuwa moto moto. Akamwambia Mo Jay kwa sauti ya mahaba, "Subiria honey nijigeuze". Husna alijigeuza kwa nyuma kumuachia msambwanda uliokithiri mpaka. 

Mo Jay akaushika na kuanza kucheza nao kwa mipapaso ya mikono yake huku Husna akitoa sauti ya huba la taratibu. "Ooooooooooiiiiiiiiiiisssssss...mmmmnnhhh....aaaaaaaaaaaaaiiiiiiisssssssshhhhhhh....Mo Jay wanitia nyege aaaaaaah..." Kijana wa watu hakuona kinyaa wala uchafu kwani alianza kuyanyonya makalio ya Husna baada ya kuipandisha sketi yake juu. 

Husna alihisi umoto moto wa ulimi na kuchanganywa na lipsi. Kwa raha anazo pewa na kuchanganyikiwa mwana mwali, Kabla ya kupoteza wakati. Husna alizidi kujitanua miguu yake na kutaka mtanange uingizwe ndani na kumwambia. "Mo Jay ingiza basi nisikie utamu mwenzio aaaaaaaaiiiiiisssssssh....Uuuuuuuuuiiiiisssssss....mmmmnh...ooooooouuuuuuuucccccchhhhh. Mmmmmmnhh...aaaaaah.. 

Kwa kawaida, Mo Jay akaifungua zipu ya suruali kwa haraka kwani utamu ulikuwa umenoga hatari. 

Akautoa mshedede na kuuzamisha ndani taratibu huku Husna akishika ukuta na kuusikilizia pindi muhongo unavyozama kwa utamu wake. Husna akaanza kutoa sauti ya mahaba kwa msikilizio wa chuma. 

Jamaa akaanza kupampu taratibu, mtanange ulizidi kuwa imara na kuanza kusugua kitumbua cha Husna. Mo Jay alipata utamu kwa kadri Husna anavyojibinua makalio yake, ndivyo hamu kuzidiana. 


ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

BLOG