Search This Blog

Sunday, April 18, 2021

RAHA YA DAFU UCHOKONOLEWE - 4

  


Chombezo : Raha Ya Dafu Uchokonolewe 

Sehemu Ya Nne (4)





“Mnh!” Maneno ya Sakina yalinirudisha kule chumbani kwa Halima ambako nililala jana yake. Nikakumbuka jinsi Halima alivyokuwa akibiringishwa na kukunjwakunjwa kama chapati huku akilalamika na kusifia kwa wakati mmoja. Kwahiyo shughuli kama ile ilikuwa na dalili zote za kuendelea huku kwa Sakina. Sasa kama anasema hayawezi kwani kuna ulazima gani?

“Yule babu wa mchana mnafahamiana?” Sakina akahoji kwa umakini.

“Mnh! Babu gani?” Nikahoji kwa mshituko kidogo kwasababu sikutegemea swali kama lile lingejitokeza ghafla kwenye mada tofauti kabisa.

“Kale kababu kalikokusaidia leo asubuhi nilipotaka kukupiga”

“A a ah hapana simfahamu” Nikajibu kwa kigugumizi.

“Mbona amekuita jina?”

“Hapana pengine alisikia wewe ukiniita”

“Mnh shoga au ndio maana umefukuzwa shule kwa kutembea na vibabu nini?” Sakina aliniuliza swali ambalo lilinisababishia kiungulia kikali kwenye chembe ya kifua na kunifanya nikohoe mara tatu mfurulizo.

Kabla ya kutoa jibu la swali lile tuligutushwa na sauti ya dirisha likigongwa kama vile ilivyofanyia usiku uliopita. Nilivuta pumzi na kuziachia kwa nguvu huku nikiwa sielewi ni kitu gani ambacho kingetokea usiku huo. Kusema ukweli sikuwa tayari kabisa kushuhudia tena uchafu kama ule niliokuwa nimeushuhudia usiku uliopita kule chumbani kwa Halima.

“Shughuli imeanza!” Sakina alizungumza huku akijigeuza kuangalia ukutani.

“Mbona hufungui sasa?” Nilihoji baada ya kumuona Sakina amejikausha utafikiri hakuwepo.

“Hayanihusu shoga” Sakina alijibu huku amegeukia ukutani.

“Sasa yanamuhusu nani? Nikahoji kwa mshangao nikihisi Dullah alikuwa amenifuata mimi usiku huo.

“Nilikwambia Dullah ni shemeji yako hukutaka kunielewa, sasa leo utakiona cha moto” Sakina alizungumza maneno ambayo sikuyaelewa kwa wakati ule na kunifanya nizidi kujawa na hofu.

Nikiwa nimetulia pale kitandani nilisikia mlango wa chumbani kwa dada Halima ukifunguliwa. Kumbe dirisha lililokuwa likigongwa lilikuwa la chumbani kwa Halima. Moja kwa moja nikagundua mgongaji alikuwa ni Dullah amekuja kutekeleza jukumu lake la kumtesa ndugu yetu.

Kwakuwa vyumba vyetu vilikuwa jirani na juu ya dari hapakuwa pamezibwa hivyo ilikuwa ni rahisi sana kunasa kila kitu kilichokuwa kikiendelea kwenye chumba cha pili. Kimya kikatawala kama kwa dakika tano hivi ndipo tukasikia sauti kama ya nyoka.

“Aaaasssh…..Aaassssahhh!” Nafikiri ilikuwa ni sauti ya dada Halima.

Sakina alikurupuka kitandani na kunigeukia mimi ambaye nilikuwa nikisali kumuomba Mungu anishushie usingizi wa kilo sita nisiweze kusikia chochote.

“Umesikia…? Umesikia sasa…?” Sakina akazungumza kwa sauti ya kunong’ona huku ametoa macho ya kishankupe.

“Ni kitu gani kwani?” Nikahoji na kujifanya sielewi chochote kile.

“Unauliza! Daktari huyo ndani ya wodi!” Akazungumza Sakina huku akichukua mto na kuukumbatia.

“Ayaaaa Baby unaweza..unaweza baba….U na we za a a!” Tukasikia sauti ya dada Halima ikizungumza kwa taabu.

“Dullah ni mwanaume mama! Dullah amebarikiwa mkono! Dullah ana nguvu! Dullah hakufanyi ukapoteza tageti na kuanza upya kama wanaume wengine!” Sakina alizungumza kwa kusifia huku akiukumbatia zaidi ule mto aliokuwa ameuweka kifuani kwake.

Maneno ya Sakina yalinifanya nikumbuke shughuli ya Dullah ambayo niliishuhudia kwa macho yangu nikiwa chumbani mwa dada Halima. Lakini pia nilikumbuka shughuli iliyofanyika mgahawani akiwa na Sakina kiasi cha kupelekea kuvunja meza ya mama pamoja na kudondosha kabati la vyombo.

“Niambie nifanye nini baba watoto wangu, sema tu nikupe nini… heti mashine yangu nambie baba” Sauti ya dada Halima ilikuwa na kimbelembele na kupenya vyema kwenye masikio yetu.

“Yani wakishaanza hivyo, hawakawii kuvunja chaga” Sakina akanogesha huku akiupapasa ule mto kama vile anampapasa mpenzi wake.

“Hivi mama anajua kweli kinachoendelea humu ndani?” Nikahoji kwa umakini.

“Anajua lakini anajifanya hajui”

“Dullah utaniangusha…sha…sha…jamani nguvu zinanishiaaaa” Sauti ya dada Halima ikasikika ikilalamika.

Sakina aliinuka pale kitandani na kusimama huku akikuna nywele zake utafikiri anawashwa na chawa. Akajivuta hadi kwenye meza iliyokuwa na vipodozi na kujitazama kwenye kioo huku akichezea nywele zake kwa kuzirudisha nyuma.

“Dullah…Dulaaah…Mume wangu leo nipe…nipe mimba mimi nitalea, mama anataka mjukuuu Ooooooh Dullah wangu shughuli unaiweza Baba” Sauti ya dada Halima ilisikika akizidi kulalamaika na kuomboleza kutokana na utamu aliokuwa anaupata kutoka kwa Dullah.

Sakina aligeuka na kwenda kujitupa tena kitandani huku akikumbatia mto wake kwa nguvu zaidi.

“Dullah wangu mbona kama leo umechanganya pilipili na sukari babaaa! Ooooh taam baby wangu!” kule chumba cha pili nako Halima alizidi kulalamika na kusifia shoo kutoka kwa Dullah wake.

Ghafla nikamuona Sakina akikata mauno huku ameukumbatia kwa nguvu ule mto na kuupiga mabusu mfurulizo.

“Mungu wangu nini hiki?” Nikajiuliza kwa mshangao huku nikimkodole macho Sakina ambaye alionekana kuchanganywa na kelele za chumba cha pili.

Sakina alitupa pembeni ule mto kisha akaanza kujitomasa mwenyewe katika sehemu mbali mbali za mwili wake.

“Ooooh baby wangu tara..tar..tatibuuu!” Sakina naye akaanza kulalamika Mungu wangu.

“Mnh haya ya leo tena mauzauza mwenzangu!” Nikazungumza kwa mshangao huku nikiendelea kumkodolea macho binti yule.

Sakina alivua khanga aliyokuwa amejifunga kisha kakamata madafu yake ya kifuani kwa mkono wa kushoto halafu mkono wa kuume akaupitisha katikati ya mapaja yake ambayo alikuwa akiyabana na kuyaachia huku akijipindu pindua kitandani.

“Dullaaa ukimaliza kwa Halima uje unipe na mimi naumiaaa mwenziooo!” Alilalamika Sakina huku akiendelea na zoezi lake.

“We Sakina unasumbuliwa na nini?” Ikabidi nihoji kwa mshangao.

“Dullah wangu ananitesa Farida” Akallamika huku akibubujikwa na machozi.

“Acha mambo ya kijinga Sakina, Dullah yupo huko anakutesaje wewe wa huku?” Nikahoji kwa mshangao.

“Farida hujui wewe na ndio maana unazungumza hivyo, mimi nampenda sana Dullah” Sakina akazungumza kwa msisitizo huku akijiinua kutoka pale kitandani.

“Utakuwa umechanganyikiwa Sakina! Utampendaje mwanaume wa dada yako?” Nikahoji kwa mshangao.

Sakina alikuwa kama vile amechanganyikiwa mtoto wa watu. Alikuja kitandani kwangu na kunikumbatia kwa nguvu huku akinimiminia takataka za mabusu ya usoni na kwenye midomo!




“Mungu wangu! Sakina unafanya manini haya?” Nikahoji kwa ghadhabu na kumsukumia pembeni.

Sakina alijiinua na kutaka kunivaa tena lakini nilimkwepa akadondokea kitandani ambako alivuta mto wangu na kuanza kuukatikia utafikiri anacheza ngoma za kizaramu.

“We Sakina umepatwa na nini leo?” Nikahoji kwa mshangao uliochanganyikana na hofu.

“Nipe Dullah wangu nipe mimi achana na Halima hajui majambozi huyo!” Sakina aliropoka huku akizidi kuuukatikia mto wangu. Nikabaki nimesimama pembeni nikimkodolea macho kama video.

“Assss aah…amnh…tamu bayen…ng’aaa ooooh!” kule chumbani kwa Halima nako mambo yalipamba moto. Nikaziba masikio yangu kwa vigaja vya mikono ili kuepuka kusikiliza zile vurugu. Hata hivyo haikusaidia kwasababu wasichana wale walijitahidi kwa kadri ya uwezo wao kuhakikisha nafaidi upuuzi wao.

Nilisikia sauti ya kitu kikivunjika kule chumbani kwa dada Hlima Kwachaaa!.Nikahisi ni lazima kingekuwa ni kitanda kimevunjwa usiku huo kwasababu vurugu za Dullah nilikuwa nazifahamu kindaki ndaki.

Baada ya sauti ile ya kuvunjika kwa kitu kule chumbani mwa Halima kimya kilitawala kwa dakika kadhaa. Lakini kule kwetu Sakina alikuwa akiendelea kujilalamisha kitandani huku akilitaja jina la Dokta Dullah.

“Aaah Dullah Bebe…niweke hivi…nataka uni..uni…uni..nakupenda saaaana” Sakina alillamika pale kitandani na kuzidi kuuchanganya ubongo wangu.

“We Sakina mbona sikuelewi! Hebu wacha upuuzi tulale!” Nikazungumza kwa msisitizo huku nikiendelea kumshangaa.

“Nakupenda Dullah! Nakupenda mimi usiendelee kunitesa tafadhali” Mwenzangu aliendelea kulalamika kwa sauti huku akiendelea kuukatikia viuno ule mto na kuupiga mabusu mfurulizo.

“Sijui nikitandike makofi ili akili yake ikae sawa?” Nikawaza huku nikihisi hasira zikinijaa kifuani.

Ghafla nikasikia mlango wa chumbani kwetu ukigongwa. Nilishituka sana na kuhofia kumuona mdogo wangu Sakina akidharirika.

“Naniiii?” Nikahoji huku nikisogea kitandani alipokuwa Sakina.

“Fungueni mimi Halima” Nilisikia sauti ya dada Halima ikizungumza kutokea mlangoni kwetu.

“Mungu wangu! We Sakina hebu wacha ujinga wako Halima amekuja” Nikazungumza huku nikimshika kujaribu kumtuliza mapepe yake.

“Niache nifaidi penzi la Dullah wangu!” Alizungumza Sakina huku akiuondoa mkono wangu kutoka kwenye mwili wake.

“Nyie fungueni mlango kwani mna biashara gani humo ndani?” Halima akapaza sauti na kuzungumza kwa ukali.

“Mungu wangu! Nisipofungua dada Halima anaweza kuwaamsha watu wengine halafu hii aibu iwe kubwa zaidi” Nikajisemea kwa hofu huku nikimuacha Sakina na kusogelea mlango.

Nilikamata kitasa na kugeuka kumtazama Sakina kwa masikitiko. Sikupenda kabisa aibu ile aliyokuwa akiifanya Sakina ionekane na mtu mwingine. Hata hivyo kwa kumsaidia zaidi nikafungua mlango.

Macho ya dada Halima yakatua kwenye kitanda changu na kumshuhudia Sakina akiwa anaendelea kujisevia kwenye mto. Halima alirejesha mcho yake kwangu na kunikazia usoni.

“Sijui amekumbwa na nini?” Nikazungumza kwa kujihami huku nikionekana kujawa na wasiwasi.

“Huyo Dullah anayemtaja ni nani?” Dada Halima akahoji kwa umakini baada ya kusikia jina la mchuchu wake likitajwa na Sakina katika mazingira kama yale.

Nilibenjua mabega juu kuashiria sikuwa namfahamu huyo Dullah aliyekuwa akitajwa.

Halima alivuta hatua hadi kwenye kitanda na kumsukuma kwa nguvu mdogo wake. Sakina akakurupuka kama vile ametoka kwenye usingizi mzito.

“Ndio nini sasa hivi?” Halima akahoji baada ya Sakina kuacha ule upuuzi wake na kuwa kama vile haelewi kitu.

“Abeee” Sakina aliitika kwa aibu.

“Inamaana wewe unamtaka Dullah wangu si ndivyo?” Halima akahoji kwa umakini mkubwa.

“Kwanini unasema hivyo dada Halima?” Sakina akahoji.

“Usiniulize mautumbo, Nimekukuta kabisa unamsololea shemeji yako halafu unafyotoka fyoto fyoto!” Dada Halima akazungumza kwa ukali huku ametoa macho kama chui aliyejeruhiwa.

“Nawewe ni lazima utakuwa unajua kinachoendelea!” Akazungumza huku amenigeukia kwa ghadhabu na kuninyooshea mimi kidole Mungu wangu




“Mbona mimi sielewi dada Halima!” Nikazungumza kwa kujihami masikini ya Mungu.

“Dullah ni shemeji yenu tena nampenda sana. Na tunakaribia kufunga ndoa, sasa ole wake mtu ajichanganye mtaelewa kwanini mama yangu ameitwa Mama Halima” Alizungumza dada Halima kwa msisitizo na kutoka chumbani mle kwa mwendo wa kudunda kama kitenesi.

Niligeuza macho yangu na kumtazama Sakina ambaye alikuwa ametawaliwa na aibu huku akitumbua macho kama mchawi.

“Utamu wa Shemeji” Nilizungumza kwa kebehi huku nikiachia tabasamu la masikitiko.

“Koma wewe!” Sakina akanijibu kwa ghadhabu.

“Toka basi kwenye kitanda changu, kazi si umeshamaliza?” Nikazungumza kwa kebehi.

“Nyoko yako!” Alinitupia tusi na kujiinua kwenda kujilaza kwenye kitanda chake huku akiwa haamini kilichokuwa kimetokea.

*****

Maisha niliyokuwa nikiishi nyumbani kwa Mama Halima yaikuwa yanaelekea kunishinda kabisa. Vituko vya watoto wake kila kulipokucha vilikuwa vimeshanichosha kwakweli. Nilitamani sana maisha ya nyumbani kwetu yaliyokuwa yamejaa heshima na hekima. Lakini ningefanya nini kwasababu yale maisha yaliyokuwa ya kishenzi ndiyo yaliyonipokea na kukubali kuishi na mimi katika wakati mgumu kama ule.

Nikiwa nafuta vyombo kwa kitambaa kule mgahawani kwetu. Sakina alifika na kunishika kwenye bega. Nilipogeuka akanikabidhi picha iliyokuwa mkononi mwake.

“Nani huyu?” Nikahoji huku nikiipokea picha ile na kuitazama kwa makini. Nilishituka kidogo baada ya kubaini kuwa ilikuwa ni picha ya Mwalimu James, yule mshenzi aliyeshiriki kuharibu maisha yangu ya masomo na kunifrakanisha na wazazi wangu.

“Huyo ndio mwanaume pekee nitakayefunga naye ndoa” Sakina alijibu huku akijitikisa kwa nyodo.

“Mnh we Sakina…” Nilizungumza kwa kuhamaki baada ya kuiona picha ile.

“Vipi mbona kama unamjua sana?” Akahoji kwa nyodo.

“Huyu…huyu…Lakini Sakina wewe!” Nikajikuta nashindwa kuzungumza neno lolote lile juu ya picha ile.

“Hapana Farida, huyu ni wa kwangu pekeyangu. Nimeachana kabisa na Dullah wenu. Sitaki tena aibu kama ile ijirudie” Sakina alizungumza kwa msisitizo huku akiinyakua picha ile kutoka mikononi mwangu na kuipiga busu kwa mbwembwe.

“Kweli atakuoa huyu?” Nikahoji kwa msisitizo.

“Huyu mwanaume angeshanioa muda mrefu tu. Sema mimi mwenyewe ndio nilikuwa namzingua kwasababu ya Dullah. Na sasa nimeamua kuachana kabisa na wanaume za watu na nimeamua kuwa na kidume changu, kwanza kina pes sana hiki” Sakina alieleza kwa ufasaha huku akiikumbatia picha ile kifuani kwake.

“We Sakina kwani kuna ulazima gani wa kuwa na mpenzi?” Nikahoji kwa umakini nikitamani kumshauri awachane kabisa na mwanaume yule kwasababu aikuwa ni mchafu wa tabia. Lakini pia nilichokuwa ninakifahamu mimi ni kwamba tayari alikuwa amemuoa Sarah.

“Sio mpenzi tuu, Mwanaume huyu amesema anataka kunioa”

“Sasa mbona hamuendani! Hebu muangalie kwanza hana hata hadhi ya kuitwa mume huyu” Nikajaribu kumvunja moyo.

“Babu nimeshapenda hivyo, wewe jiandae kula wali wa harusi”

“Kusema kweli wala hanibariki mimi, kama ni lazima sana bora utafute mwanaume mwengine” Nikazungumza kwa kebehi.

“Unataka akubariki kwani anakuoa wewe, acha wivu wa kishamba wewe!” Sakina akazungumza kwa jazba.

Sauti ya mtu aliyekuwa akijikohoza ilitukatisha mazungumzo yetu na kutupa macho mgahawani. Tukabaini kulikuwa na mteja ameingia muda huo.

Sakina alitaka kwenda kumsikiliza mteja yule lakini alipomtazama vizuri akasita kumsogelea na badala yake akarejea kule jikoni.

“Vipi mbona unarudi?” Nikahoji.

“Kichefuchefu chako hicho kimefika” Alizungumza Sakina kwa sauti ya chini huku akiendelea na shughuli yake.

“We Sakina mbona unanitisha! Ni nani kwani?” Nikahoji kwa mashaka.



“Ni kile kibabu chako nenda ukakasikilize mimi kitanichefua bure” Alizungumza Sakina kwa sauti ya kunong’ona.

“Kibabu gani?”

“We nenda utakutana nacho hukohuko” Alizungumza kwa msisitizo.

Nilivuta pumzi na kuziachia kisha nikainuka na kwenda kule mgahawani kukiangalia hicho kibabu nilichoambiwa nafahamiana nacho.

“Mungu wangu kumbe ni wewe!” Nilijikuta nikizungumza kwa kuhamaki baada ya kumkuta mzee Makwacha ameketi pale mgahawani huku ameachia tabasamu baada ya kuona sura yangu.

“Nataka Chai maharagwe” Babu yule alizungumza huku akicheka.

“Chai maharage au maharagwe?” Nikahoji kwa utani na kugeuka kuelekea jikoni huku nikitabasamu kwa furaha.

“Nyoo mtoto mdogo unajibebesha vizee! Vitakufia laana wewe!” Sakina akazungumza kwa utani huku akicheka baada ya kuniona nikiingia jikoni kuandaa chakula cha mzee Makwacha.

“Vizee vinajua kubembeleza havileti presha” Nikazungumza kwa utani huku nikipakua maharage kwenye bakuli.

“Lakini kweli mwenzangu maana tunaojifanya kupenda vijana kila siku tunalizwa”

“Utajiju na vijana wenzako” Niijibu na kutoka jikoni mle huku Sakina akinisindikiza kwa kicheko cha kishambenga.

Nilikwenda moja kwa moja hadi alipokuwa ameketi mzee Makwacha na kumuandalia kifungua kinywa halafu nikaketi kwenye kiti cha jirani yake, tukawa tunatazamana.

“Haya niambie umenusurika vipi kutoka kwenye mikono ya dola?” Nikahoji kwa msisitizo na umakini mkubwa.

“Sikuwa na kosa na ndiomaana nimeachiwa huru”

“Umeaminika vipi yani?”

“Wamekosa ushahidi juu ya kile walichokuwa wananituhumu” Alizungumza mzee Makwacha huku akipeleka kijiko cha maharage mdomoni.

“Hakika Mungu ni mwema. Utalipwa kwa kila wema ulioutenda Babu” Nilizungumza kwa hisia kali huku nikiinua mikono juu kumshukuru Muumba kwa kile alichokuwa amekitenda kwa mzee Makwacha.

“Nimepata taarifa kuwa umefukuzwa nyumbani” Mzee Makwacha alizungumza.

“Yaani Babu we acha tu. Baba yangu hataki hata kuniona kwaababu ya yule firauni mmoja” Nikazungumza kwa jazba.

“Hakuna marefu yasiyo na ncha mjukuu wangu”

“Mwenzetu ameshikilia mpini hatuna la kufanya” Niakazungumza kwa sauti iliyokata tamaa.

“Hapana usikate tamaa, lazima tulipe kisasi na tufichue uchafu wake wote” Mzee Makwacha akaungumza kwa msisitizo.

“Tutafichuaje sasa wakati mimi na wewe sote hatupo shuleni pale” Nikazungumza kwa sauti iiyopoteza matumaini.

“Unapenda kurudi kwa wazazi wako na kuendelea na masomo?”

“Hata sasa hivi natamani sana muujiza huo utendeke”

“Basi ni lazima tupambane” Mzee Makwacha alisisitiza.

“Unajua amemuachisha shule Sarah na anaishi naye kinyumba” Nikazungumza.

“Sarah ni yupi?”

“Kale kasichana nilikokuwa napigana nako siku ile ya tukio”

“Ahaaa nimemkumbuka”

“Sasa wanaishi pamoja kama mke na mume”

“Wanaishi wapi?”

“Sijajua, lakini nilikutana nao wakanieleza hivyo”

“Au wamekudanganya tu ili wakuumize akili?”

“Hapana Babu, kwa jinsi nilivyowaona ni kweli wanaishi pamoja”

“Safi, huo ni mwanzo mzuri” Babu alizungumza kwa matumaini makubwa.

“Lakini pia amemtongoza huyu binti ninayefanya naye kazi hapa”

“Usinambie we mtoto!”

“Na huyu binti anaonekana kumkubali kwasababu ameahidiwa ndoa” Nikaeleza.

“Hakika huyu kijana ni firauni! Sasa wewe vumilia wakati mikakati yetu inaendelea” Mzee yule alieza.

Nilivuta pumzi na kuziachia huku nikikuna nywele zangu za nyuma ya kichwa. Sikuelewa kuvumilia kule alikoniambia alikuwa anamaanisha ni uvumilivu wa muda gani kwasababu binafsi maisha ya nyumba ile yalikuwa yamenichosha.

“Vipi mbona kama kuna kitu hakipo sawa?” Mzee Makwacha akahoji kwa umakini.

“Babu hapa naishi vizuri lakini tabia za ndugu zangu ni chafu mnoo!” Nikazungumza kwa sauti ya chini huku nikiangalia kule kwenye mlango wa kuingilia jikoni kuhakikisha Sakina hasikii mazungumzo yetu.

“Sasa tunafanyaje mjukuu wangu?”

“Nitavumilia kama ulivyosema lakini kwakweli maisha ya hapa ni ya kishenzi” Nikazungumza kwa unyonge.

Mzee Manyanga aliinamisha kichwa chini kwa sekunde kadhaa kisha akainuka huku sura yake ikiwa imepambwa kwa tabasamu la matumaini. 



“Utakuwa tayari kujihifadhi sehemu kama mfanya kazi wa ndani?” mzee Makwacha alihoji.

“Kama kuna amani na heshima nitakuwa tayari Babu kuliko hapa”

“Basi kuna mama mmoja ambaye nalinda ofisi yake alikuwa anahitaji mfanyakazi wa ndani” Alieleza mzee Makwacha.

“Sawa nitakuwa tayari. Utakuwa umenisaidia sana kuondokana na mabalaa ya nyumba hii” Nikazungumza kwa matumaini makubwa.

Mzee Makwacha alimimina maji kutoka kwenye jagi kisha akapeleka kinywani na kusukutua mara mbili kabla ya kumeza. Aliingiza mkono mfukoni na kutoa kalamu na karatasi kisha akaandika.

“Chukua hii namba yangu ya simu, tutawasiliana kwa kila hatua” Alizungumza Mzee Makwacha alipokuwa ananikabidhi kipande cha karatasi.

“Sawa Babu” Nikakipokea

“Kwaheri..” Akazungumza huku akijiinua na kutoka mgahawani mle akiniacha na matumaini mapya.

“We mama kama Bebe wako ameondoka njoo tufanye kazi usitegee huko” Sakina aliniongelesha baada ya kubaini kuwa mzee Makwacha aikuwa ameshaondoka mgahawani pale.

Nilirudi jikoni na kuendelea na shughuli za siku hiyo. Ndani ya moyo wangu nilihisi hali ya matumaini baada ya kukutana na mzee Makwacha na kuahidi kunisaidia kutoka katika ile hali ngumu niliyokuwa nakabiliana nayo.

Tukiwa tunaendelea na maandalizi ya kifungua kinywa kwa siku hiyo, tukasikia viti vikisogezwa mgahawani kuashiria kuwa kulikuwa na mteja anahitaji huduma. Niliamka haraka na kuchungulia kwenye kadirisha kadogo kutokea jikoni na kujikuta nikitetemeka mwili.

Nilimtazama Sakina kwa jicho la tahadhari na kutamani sana asimuone mteja yule lakini alinishitukia na kuja kuchungulia mwenyewe.

“Mungu wangu!” Sakina alizungumza kwa kuhamaki huku akivuta hatua kutaka kwenda kumlaki mteja wetu lakini nilimdaka mkono na kumvuta kidogo.

“Ngoja niende mimi” Nikazungumza kwa tahadhari.

“Hapana Farida, hii ni nafasi muhimu sana kwangu” Sakina alizungumza na kujichomoa kutoka mkononi mwangu ghafla na kusogea nyuma hatua mbili.

“Kuwa makini Sakina huyo sio binadamu wa kawaida” Nilizungumza kwa msisitizo huku nikihisi mapigo ya moyo yakidunda kwa kasi.

“Acha wivu wa kijinga kenge wewe!” Sakina alizunguma na kutoka jikoni kuelekea kwa mteja wake.

Ndugu msomaji unaweza usiamini lakini mteja aliyekuwa amefika mgahawani wakati ule alikuwa ni Mwalimu James. Mwanaume ambaye alinionesha kwenye picha kuwa ameamua kuwa naye kimapenzi. Huyo Mwalimu James ndio yule ambaye nilitambulishwa na Sarah kuwa wamefunga ndoa. Kwakweli sikuelewa kabisa ningefanya kitu gani ili kumuokoa ndugu yangu yule. Nilihofia kama ningekurupuka lazima Sakina angenichukia na kuhisi namtaka mwanaume wake. Nikajibanza sambamba na dirisha kuweza kunasa mawili matatu.

“Leo hukwenda kazini Baba” Sakina alizungumza kwa sauti ya kubania puani.

“Jumapili hatufanyi kazi mrembo”

“Haya karibu sana, naona leo umenikumbuka asubuhisubuhi” Sakina alizungumza huku akijiweka pembeni mwa Mwalimu James.

“Ndio ujue kuwa nakupenda sana mtoto mzuri” Mwalimu James akaunguruma.

“Mmnh nyie wanaume si ndivyo mnavyosemaga”

“Mimi sipo kama hao. Tena nawachukia sana wanaume wenzangu wanaotenda dhambi ya uwongo hasa katika mapenzi” Mwalimu James akazungumza kwa msisitizo huku akipeeka mkono wake na kupapasa sehemu za kwenye paja la Sakina.

“Yaani nyie wanaume mkimtaka mwanamke mnakuwa weeema lakini mkishakipata tu mnachokitaka mnasepa mazima” Sakina akazungumza huku akionekana kujawa na aibu.

“Sasa tukubaliane kitu kimoja..”

“Enhe nakusikiliza zungumza tu”

“Mimi nataka tusifanye kitu chochote hadi tutakapofunga ndoa. Hapo vipi?” Mwalimu James akazungumza kwa kujiamini huku akiuondoa mkono wake kutoka kwenye paja la mguu wa Sakina.

“Kama ni hivyo naanza kukuamini. Basi tusifanye kitu hadi tutakapofunga ndoa kama ulivyosema” Sakina akazungumza kwa kudeka huku akijawa na faraja ya kupata mwanaume kutoka mbinguni.

Niliposikia kauli ya Sakina nilihisi kitu kikinichoma tumboni kama mshale. Nilishika tumbo na kuketi chini huku nikiugulia maumivu yale. Mazungumzo ya Sakina na Mwalimu James hayakuwa yamenibariki kabisa. Nikatamani kuwavamia na kuwafurumusha kwa kuwatandika na mwiko wa kusongea ukali.

“Nakupenda sana Sakina, tukishafunga ndoa hakika tutaishi kama Malaika” Mwalimu James alizungumza.

“Lakini Babe umesema tusifanye kitu hadi tutakapofunga ndoa si ndivyo?” Sakina akahoji kwa sauti ya kudeka.

“Nakuahidi mchumba kwamwe sito gubugudhi kwa hilo hata siku moja” Mwalimu akazungumza kwa msisitizo.

“Kwamfano nikiomba je itakuwaje?”

“Yaani ukitaka wewe?”

“Ndio kwamfano nikishikwa na hamu utaweza kunipa?”

“Wewe ni Malkia wangu, nitafanya chochote kile ilimradi nikufurahishe mrembo wangu” Mwalimu akazungumza huku akionekana kufurahishwa na maneno ya Sakina.

“Haya niambie sasa unakuja kunioa lini?”

“Ngoja nijipange kwaajili ya kuja kutoa posa hivi karibuni”

“Usije ukanitenda lakini, mwenzio naogopa sana kuumizwa na mapenzi” Sakina alizungumza kwa tahadhari.

“Unajua sijawahi kupenda kama ninavyo kupenda Sakina wangu. Lakini pia sijawahi kuwa na mahusiano na mtu yeyote yule hivi karibuni” Mwalimu James alizungumza kwa hisia kali huku akiwa amempakata Sakina kwenye mapaja yake na kuchezea nywele za binti yule.

Maneno ya Mwalimu James yalizidi kunipandisha hasira kule jikoni na kunifanya nishindwe kuvumili. Nikaangalia kulia na kushoto kuona kama ningeona silaha yoyote ile. Nilivuta hatua hadi mezani na kuchukua sufuria mbili za kupikia maharage, nikatoka nazo pale mgahawani walipokuwepo Sakina na Mwalimu James.

Nikiwa nimezikamata sufuria zile moja mkono wa kulia na nyingine mkono wa kushoto nikazigonganisha pamoja kwa hasira na jazba na kutokea mlio kama wa bomu la Mbagala ‘Pa a a a a!’



Wawili wale walikurupuka utafikiri wamefumwa wakiiba miwa kwenye shamba la mihogo. Mwalimu James alisimama wima huku ametoa macho utafikiri ameona jua usiku wa manane. Hakutegemea kama angeweza kukumbana na shambulio kama lile.

“Haa wewe!” Mwalimu James akashangaa zaidi baada ya kuiona sura yangu.

Wakati wawili wale walipokuwa wamekumbwa na mshangao wa dharura mtoto wa kike nikavuta mkono wa kuume na kuachia sufuria moja kumlenga Mwalimu James. Nilikuwa nimekusudia kumbamiza maeneo ya kichwani lakini kwa bahati mbaya kwangu ama nzuri kwakwe alikwepa na sufuria ile ikapiga ukutani Pa ta a a!

“Farida unafanya nini?” Sakina akahoji kwa kuhamaki huku akihisi nilikuwa nimepandwa na kichaa.

“Tulia Sister nikuokoe kutoka mikononi mwa firauni huyo!” Nilizungumza kwa sauti ya upole huku nikirusha tena sufuria niliyobaki nayo na hakika Mungu ni mwema kwani nilifanikiwa kumtandika Baba wawatu kwenye paji la uso Ti i i i !

“Yalaaaa!” Mwalimu James alitoa ukelele wa maumivu huku akijishika kwenye paji lake la uso na kujifuta damu.

“Kufa Nyanga’u we!” Nikatamka kwa jazba.

Sakina alipoona vile akajawa na upepo kifuani kwa hasira na kuvimba kama chura ndani ya dimbwi la tope. Akauma meno ya chini kwa ghadhabu kisha akavuta hatua kunifuata kwa lengo la kuhakikisha siku hiyo adabu inanikaa sawa.

“We chokoraa leo nakutoa roho!” Sakina alizungumza alipokuwa akinisogelea kwa spidi roketi.

Niliangalia kulia na kushoto na kufanikiwa kuokota chupa ya soda iliyokuwa pembezoni mwa mlango wa kuingilia jikoni. Nilipiga chini chupa ile na kubakiwa na kipande mkononi huku nikiwa nimetumbua macho kumsubiria Sakina kwa mapambano.

“Haya tuliza kiranga chako! Ukisogea tu nakutufua utumbo” Nilizungumza kwa tahadhari huku nimeshikilia ile chupa kwa ukakamavu.

“Sakina mpenzi wangu usiende atakufua kweli huyo hazimtoshi vizuri!” Mwalimu James alizungumza kwa tahadhari baada ya kuniona nimecharuka mtoto wa kike.

“Na wewe unasemaje? Nisubiri nikuoneshe kilichomtia kanga madoa!” Nikazungumza kwa ghadhabu huku nikivuta hatua kumfuata Mwalimu James pale alipokuwa amesimama. Kudadadeki! Nilimshuhudia mwanaume yule akitoka nduki na kupotea kama upepo katika mazingira yale.

“Nyoo! Mwana laana, mjaa laana, mjukuu wa shaitwana uliyelaaniwa na Maulana!” Sauti ya Mama Halima ilinigutusha nilipokuwa nikimtimua yule firauni kutoka pale mgahawani.

“Mama unaona tabia yako ya kuokota majitu na kutuletea ndani. Safari hii umetuletea zombi linakunywa damu za watu” Sakina akazungumza baada ya kumuona mama yake akizungumza kwa hasira.

“Mama..” Nikaita kwa kuhamaki.

“Koma nani mama yako! Nimekusaidia halafu unajifanya bondia kuchapa wateja wangu!” Mama Halima alizungumza kwa ghadhabu.

“Mama yule sio mteja. Yule ni….”

“Kelele shangingi wewe! Sitaki kukuona tena katika macho yangu” Alizungumza mama Halima.

“Naomba unisamehe mama sikuwa na nia mbaya, yule mwanaume….”

“Tena mama huyu ngadu anampango wa kumchukua Dullah wa dada Halima” Sakina akazungumza.

“Unasemaje? Yaani wewe piipili hoho umefadhiliwa unalipa utopolo” Mama akazungumza kwa hasira zaidi.

“Sio kweli mama” Nikaungumza kwa upole na unyenyekevu wa haliya juu.

“Tulipokusaidia mpendwa panatosha. Nenda ukakusanye virago vyako utafute chaka lingine" Mama Halima akazungumza kwa msisitizo.

“Nisamehe mama” Nikazungumza huku nikipiga magoti na machozi yakinitiririka kwenye mashavu yangu. Hakika nilijutia kile nilichokuwa nimekifanya kwa Mwalimu James. Sikufikiria kama yangeweza kufikia hatua kama ile. Hakika wa moja havai mbili.

“Kwanini unakuwa mgumu kuelewa mtoto, au unataka tukutoe kwa mateke na ngumi kama unavyowafanya wateja wangu?” Mama Halima alizungumza kwa ghadhabu huku akiwa ameshika kiuno.

“Si uondoke kwani kwenu hapa?” Sakina akadakia.

“Toka bibi usije ukatuharibia biashara buree! Nimegundua kwanini nimeyumba kibiashara 



*****

Hakika Mungu ni mwema na anapaswa kushukuriwa wakati wote. Nilifanikiwa kuondoka pale nyumbani kwa Mama Halima na kwenda kuanza maisha mapya na mtu mwingine kabisa aliyefahamika kwa jina la Manka.

Dada Manka alikuwa ni mwanamke ambaye hakuwa mtu mzima lakini kutokana na cheo alichokuwa nacho kazini walizoea kumuita Madam. Mzee Makwacha alikuwa ni miongoni mwa watu waliokuwa wakifanya kazi pamoja na Madam ambapo yeye alikuwa mlinzi wa ofisi ile ya utamaduni.

Nakumbuka siku niliyokuwa nimekutanishwa na Madam Manka kwa mara yakwanza, mzee Makwacha alimueleza kuwa mimi nilikuwa ni mjukuu wake ambaye nilitokea kijijini na kuja mjini kwaajili ya kufanya kazi za ndani.

Madam alinipokea kwa heshima kubwa ya mzee Makwacha na kumuahidi kuishi na mimi kama vile mdogo wake wa kuzaliwa naye. Hivyo akamtaka mzee yule kuondoa wasiwasi kabisa juu yangu.

Nakumbuka nilipoingia ndani ya nyumba ya mwanamama yule nikabaini utofauti mkubwa uliokuwepo kati ya maisha ya mama Halima na maisha ya Madam Manka, hasa ukubwa wa nyumba pamoja na vitu vya gharama vilivyokuwemo ndani ya nyumba ile.

“Karibu sana mdogo wangu, jisikie upo nyumbani” Madam Manka alinieleza kwa sauti ya upendo.

“Asante sana dada Manka” Nikajibu kwa heshima.

“Humu ndani tunaishi watu watatu na wewe utakuwa wa nne"

“Ndio dada” Nikaitika huku nikijaribu kutafakari tabia za hao viumbe wengine ambao wanaishi ndani ya nyumba ile.

“Tunaishi mimi, mume wangu pamoja na wifi yangu” Madam Manka alizungumza kwa sauti ya upole.

Niliitika kwa kichwa huku nikijiweka vizuri kwenye kochi nilipokuwa nimeketi. Mazingira yale yalinikumbusha mazingira ya nyumbani kwetu Mwananyamala. Hata hivyo kwakuwa babu alinitambulisha kuwa nilikuwa natokea kijijini hivyo nikajifanya mshamba na muoga hasa.

“Shikamoo Madam” Sauti ya msichana akisalimia dada Manka ilinigutusha na kugeuza macho yangu kumuangalia.

“Karibu kuna mgeni njoo nikutambulishe” Madam Manka alizungumza kwa bashasha na yule msichana aliyesalimia.

Ndugu msomaji unaweza usiamini nilichokuwa nakishuhudia ndani ya nyumba ile. Msichana aliyemsalimia Madam alikuwa ni Sarah.

“Kutana na Farida atakuwa na sisi hapa nyumbani tukisaidiana naye kazi za hapa na pale” Madam Manka alinitambulisha kwa sauti ya upendo mbeleya msichana firauni Sarah.

“Ahaa karibu Farida. Kuwa na amani” Sarah akanikaribisha utafikiri alikuwa hajawahi kuniona hata siku moja katika maisha yake.

“Farida mdogo wangu..” Madam aliita

“Abee”

“Huyu ndio yule wifi yangu niliyekwambia. Yeye anaitwa Agnes” Alizungumza Madam kwa ile sauti yake ya upendo.

Lile jina la Agnes lilinishitua kidogo na kunifanya nipaliwe na mate na kupelekea kukohoa mfurulizo.

“Pole jamani Farida wetu” Sarah akazungumza kwa sauti ya upendo.

“Nenda kamletee mwenzako maji ya kunywa” Madam alizungumza huku akionekana kujawa na wasiwasi kutokana na kule kukohoa kwangu.

Sarah alikunja kidogo sura kuonesha kutokuridhishwa na kitendo kile cha kuniletea maji ya kunywa. Hata hivyo alifanya kama alivyoagizwa na wifi yake.

Ndugu msomaji nisikufiche nilikuwa katika wakati mgumu sana kwa kile kitendo cha kukutana na Sarah ndani ya nyumba ile. Inamaana kumbe nilikuwa nakwenda kufanya kazi za ndani kwenye nyumba ya wakina Sarah! Nikahisi kama vile nimeruka mkojo na kwenda kukanyaga kinyesi kwa makusudi.

“Mkosi gani huu?” Nikajiuliza kimoyomoyo nilipokuwa napokea maji ya kunywa kutoka kwa Sarah.

“Agnes utamuonesha mwenzako mazingira mbalimbali mimi nakwenda kupumzika kidogo” Madama alizungumza na kujiinua kutoka kwenye kochi.

“Hamna shida Madam nitahakikisha kilakitu kinakaa sawa” Sarah alizungumza huku akiachia tabasamu la faraja na upendo.

“Nakuaminia my Wii” Madama alizungumza hukuku akivuta hatua kuelekea chumbani mwake na kutuaha mimi na Sarah pale sebleni.

Niliinua birauli ya maji ya kunywa kwa lengo la kupiga funda mbili tatu lakini Sarah akanipokonya maji yale.

“Nyoo huna haya wewe! Kwako hapa?” Sarah alizungumza kwa kebehi huku akiwa ameshika ile birauli ya maji ya kunywa.

ENDELEA…35

“Sara…” Nikaita kwa kuhamaki.

“Koma mimi siitwi Sarah! Yule mshenzi mwenzio amekwambia naitwa nani?” Sarah alizungumza maneno ambayo hayakuniingia akilini hata kidogo.

“Samahani mpendwa jina la Sarah ndio nimelizoea”

“Sasa inakubidi uwache mazoea na ukome kunifahamu. Mimi na wewe hatujawahi kuonana hata siku moja” Alisema Sarah kwa msisitizo.

“Sawa nimekuelewa” Nikajibu kwa upole huku nikiona wazi kulikuwa na kitu hakipo sawa pale ndani.

“Haya sema ni kitu gani kimekuleta hapa?” Sarah akahoji huku ameshika kiuno.

“We unaniuliza kama nani?” Nikahoji kwa jazba baada ya kumuona anataka kunipanda kichwani mapema kiasi kile.

“Mama mwenye nyumba” Sarah akajibu kwa ufupi.

“Sawa mama nimekuja kufanya kazi za ndani” Nikajibu kwa upole na kujitahidi kuzuia hasira zangu.

Lile jibu langu lilimfanya Sarah kuangua kicheko kwa sauti utafikiri alikuwa ameona kitu gani sijui.

“Usinichekeshe wewe. Inamaana nyumba zoote hizo hukuziona hadi uje kufanya kazi nyumbani kwangu mimi?” Alihoji Sara huku amenishikia kiuno.

“Lakini Sarah mimi nimekuja nyumbani kwa Madam sio nyumbani kwako!” Nikajikuta nikizungumza kwa umakini.

“Eboo! Hivyo ndivyo alivyokudanganya? Makubwa haya!” Sarah akazungumza na kwenda kujitupa kwenye kochi huku akitupa mikono na miguu kulia na kusho kama vile alikuwa amechoka sana.

“Naomba unioneshe hayo mazingira nifahamu majukumu yangu” Nikazungumza kwa kusihi.

“We kuku nini! Inamaana upo hapa halafu hujui majukumu yako?” Sarah akahoji kwa kebehi.

“Nayajua majukumu yangu na ndiomaana nahitaji kuelekezwa ili niifahamu mipaka yangu” Nikazungumza kwa msisitizo.

“Hadi muda huu umeshavuka mipaka yako”

“Kivipi sasa?”

“We unangea na mama mwenye nyumba utafikiri unazungumza na mtoto mwenzio!” Sarah alizungumza kwa kebehi.

“Najua wewe ni mwenyeji wangu na ndiomaana nahitaji ushirikiano wako” Nikazungumza kwa sauti ya kusihi.

“Shika adabu yako wewe mtoto! Unaniita mwenyeji wako nimekuleta mimi hapa?” Akazungumza kwa jazba.

Nilivuta pumzi na kuziachia kwa mkupuo huku nikikumbuka maisha ya upendo niliyokuwa nimeyakimbia kule Makumbusho kwa mama Halima. Nikaona wazi kuwa niliruka mkojo na kukanyaga kinyesi.

“Subiri huyo mende mwenzio aliyekuleta hapa ndio akuelekeze shughuli za kufanya” Alizungumza Sarah kwa nyodo.

Nakwambia mtoto wakike mbona umbea ulikuwa umeniisha. Nilitamani kuaga muda uleule ili kumuepuka shetani yule ambaye alishiriki kwa kiasikikubwa sana katika kufukukuzwa kwangu shule na kuishia kuishi maisha ya kutangatanga kama mbayuwayu.

Mara tulisikia sauti ya mlango wa kutokea nje ukigongwa taratibu. Mimi na Sarah tukatazamana kwa sekunde kadhaa pasipokusema neno.

“Haya fungua mlango. Hilo ni moja ya jukumu lako” Sarah akazungumza kwa msisitizo.

“Lakini Sarah…” Nikataka kujitetea.

“Hakuna cha lakini, kama unataka kazi fungua mlango” Akazungumza kwa msisitizo.

Huku nikiwa na hofu kubwa ya kukutana na mzee mwenye nyumba nikajiinua kutoka kwenye kochi na kuuendea mlango. Nilikamata kitasa na kugeuka nyuma kumuangalia Sarah.

“Fungua mlango! Unaogopa nini sasa?” Sarah akasisitiza.

Niliomba Mungu anipe ujasiri. Nilizunguusha funguo kisha nikanyonga kitasa kufungua mlango ule. Mungu wangu! Mtu aliyekuwa akigonga mlango ule alikuwa ni Mwalimu James.

“Tukusaidie nini?” Nikajikuta nikihoji kwa ghadhabu.

Mwalimu James alikuwa kama vile panya amenaswa kwenye mtego wa gundi. Hakuelewa swali langu wala hakuelewa kilichokuwa kinaendelea kwa wakati ule. Akanitazama vizuri kuhakikisha sikuwa na yale masufuria yangu niliyombamiza nayo usoni kule mgahawani kwa Mama Halima.

“Usinitumbulie mimacho sema nikusaidie nini?” Nikahoji kwa msisitizo zaidi na kushindwa kuficha hasira zangu mbele ya mwanaume yule aliekuwa amesimama mbele ya macho angu.

“Naomba niingie ndani” Mwalimu James akazungumza kwa sauti ya upole huku akimeza mate kwa taabu. Alipeleka kiganja cha mkono usoni mwake kushika ile sehemu niliyokuwa nimeutandika na sufuri kule mgahawani.

“Uingie ndani nyumba yako hii?” Nikahoji kwa ghadhabu.

“Farida…!” Mwalimu James akajikuta amezungumza kwa jazba na hasira.

“Farida wa nyoko! Potea haraka kabla sijakuamshia tifu nadhani unanifahamu vizuri” Nikaendelea kumpiga mkwara mshenzi yule, maana niliona anazidi kunifuata fuata kila nilipokuwa nakwenda. 

Haya tena mambo ndio yameanza upyaaaa! Sasa na huyu nyumbu mwingine sijui ametokea wapi? watanitoa roho Mungu wangu



Nilijikuta nikisukumwa kidogo kutoke anyuma na kunifanya nipepesuka hadi kwenye kochi lililokuwa jiranina mlango.

“Karibu Laazizi nyonga mkalia ini” Sarah alizungumza baada ya kunisukuma na kusimamayeye mlangoni.

“Nikitu gani kinaendelea hapa ndani?” Mwalimu James akahoji kwa mashaka kwasababu hakutehgemea kabisa kukutana na mimi katika mazingira kama yale.

“Huyu ndio yule House gilr ambaye Madam alisema atatuletea” Sarah akazungumza kwa nyodo maneno ambayo yalinifanya nianze kuhisi kizunguzungu. Inamaana ni kweli nyumba ile ilikuwa ni ya Sarah na Mwalimu James? Sasa mbona Madam aliniongopea na kusema ni nyumbani kwake!

Sauti za kandambili zilisikika zikiburuzwa kutokea kwenye chumba cha Madam kuelekea sebleni. Nikawaona wawili wale wakiachiliana na kila mmoja akaketi kwenye kochi lake.

“Karibu mume wangu, umefika muda mrefu sana?” Madam alizungumza huku akivuta hatua kulekea kwenye kochi alilokuwa ameketi mwalimu James.

“Hapana ndio naingia hivi” Mwalimu James akajibu huku akionekana kujawa na uchovu.

“Pole sana mume wangu” Madam alizungumza na kumpiga busu la kwenye paji la uso mwalimu James.

Wakati wote huo Sarah alikuwa ametulia akijifanya amezama kuangalia runinga. Na mimi nikawa najibaraguza ili nisionekane kama nilikuwa nashuhudia mauza uza ya ndani ya nyumba ile.

“Naona tuna mgeni” Mwalimu James alihoji huku akinitazama kwa kuibia.

“Yeah ni kweli anaitwa Farida” Madam alizungumza huku akiwa ameketi pembeni mwa Mwalimu James.

“Okay”

“Ndio yule dada wa kazi niliyekwambia”

“Ahaa karibu sana Frida” Mwalimu James akazungumza huku akitabasamu.

“Sio Frida, anaitwa Farida” Madam akazungumza kwa msisitizo.

“Ooh sory! Karibu Farida” Mwalimu James akajifanya kusahihisha.

“Farida huyu unayemuona hapa ndio mume wangu, na ndio baba wa mjengo huu” Madam alizungumza kwa msisitizo huku akiachia tabasamu la amani na upendo.

Ndugu msomaji nakwambia nilijikuta katika wakati mgumu kila dakika zilivyosonga mbele. Yaani yule firauni ambaye nilikuwa na mpango wa kulipa kisasi leo hii anakuwa bosi wangu? Aisee unaweza usiamini kabisa.

“Naona Agnes amefurahi sana kupata mwenzake” Mwalimu James alizungumza huku akitabasamu na kunitupia chicho la kuibia.

“Kabisa, yaani ukiupasua moyo wangu utakuta mafuraha yanamiminika tu moyoni mwangu” Sarah akazungumzahuku akijichekesha kinafki mbele ya Mwalimu James na Madam.

“Basi na wewe wifi yangu ukae vizuri na mwenzako” Madam akazungumza kwa umakini wa hali ya juu.

“Hakuna shida Madam, yaani muda mfupi tu mgeni wetu ameshanifurahia na amenipenda” Sarah alieleza kwa furaha huku akinitazama.

“Heti Bibie yasemwayo yamo kweli?” Mwalimu James akahoji huku akinitazama.

“Hakika nampenda sana, hana shida yoyote” Nikajibu huku nikionekana kujawa na aibu.

“Haya nendeni mkaandae chakula cha jioni” Madam alizungumza akituamrisha mimi na Sarah.

“Twende jikoni mpendwa wangu” Sarah alizungumza huku akinizawadia tabasamu zito la upendo.

Tuliondoka na kuwaacha Mwalimu James na Madam sebleni wakionekana kufurahia ujio wangu ndani ya nyumba ile.

****

Kutokana na mtihani mzito niliokuwa nimekutana nao ndani ya nyumba ile, ilibidi nimtafute mzee Makwacha haraka sana kupitia namba ya simu aliyokuwa amenipatia. Nilitamani sana anipe ushauri na kama ikiwezekana niondoke kwenye nyumba ile.

Jambo la ajabu ni kwamba mzee Makwacha hakushangazwa na taarifa nilizompatia na badala yake akanifahamisha kuwa yeye alikuwa anaelewa kila kitu na alidhamiria kunipeleka mimi katika mazingira yale. Hivyo mzee yule akanipa mbinu na mikakati ya kufanikiwa malengo yetu. Maneno ya mzee yule yakanipa moyo wa kupambana.

Maisha mapya kama dada wa kazi za ndani niliyapokea kwa moyo mmoja ndani ya nyumba ile ya Madam na Mwalimu James. Hata hivyo bado sikuwa nimepata jibu la kutosha juu ya uhusiano wa Sarah na Mwalimu James. Madam alinieleza kuwa Sarah ni ndugu wa Mwalimu James lakini Sarah mwenyewe alinieleza kwa maneno na vitendo kuwa yeye ni mke wa Mwalimu James. Hivyo hatua ya kwanza ilikuwa ni kuutafuta ukweli wa jambo hilo.

Nakumbuka nilikuwa nikiandaa kifungua kinywa kwaajili ya Mwalimu James na Madam kabla hawajakwenda kazini. Nikiwa nimesimama pembeni ya meza ya chakula nikahisi mtu ananishika kiunoni jambo lililosababisha nishituke kwa nguvu.

“M a m a a a a!” Nikapaza sauti kwa hofu.



“Oooh pole mrembo sijakusudia kukushitua” Alizungumza Mwalimu James kwa sauti ya kubembeleza.

“Kumbe ni wewe!” Nikazungumza kwa aibu baada ya kubaini kuwa alikuwa ni Mwalimu James.

“Hakika Mungu ni mwema” Mwalimu James alizungumza huku akivut kiti na kuketi.

“Najua…” Nikajibu huku nikicheka cheka.

“Unajua nini?”

“Najua kuwa Mungu ni mwema na ndiomaana ametukutanisha tena” Nikazungumza kwa tabasamu.

Kauli yangu ilionekana kumuingia mwalimu James na kumsisimua kiasi cha kutulia kama vile alikuwa amemwagiwa maji ya barafu mwilini. Alivuta pumzi na kuziachia kwa nguvu kisha akameza funda la mate kwa taabu.

“Vipi mbona kama umekufa” Nikahojikwa sauti ya mahaba mtoto wa kike. Shule niliyoipata kule nyumbani kwa Mama Halima ilitosha kunifanya niwe bingwa wa mitego.

“Hapana Farida nipo hai!” Akazungumza kwa kukurupuka.

“Huwezi kujua alichokipanga Mungu kati yangu mimi na wewe” Nikazungumza kwa sauti ya chini.

“Hata mimi nahisi kuna kitu Mungu ametupangia” Mwalimu James alizungumza huku akinitazama kwa jicho la uchu.

“Sijui ni kitu gani?”

“Nahisi ni mapenzi”

“Na kama ni mapenzi, hakika yatakuwa ni mapenzi ya dhati” Nilizungumza huku nikiachia tabasamu na kurembua macho.

“Nashukuru Mungu kama umeligundua hilo” Akazungumza huku akiuma mdomo wa chini kwa meno ya juu na macho ameyafinya kidogo kuashiria msisitizo.

“Siku zote penye ukweli, uwongo hujitenga” Nikasema huku nikimimina chai kwenye kikombe.

“Usitake ninenepe hadi nipasuke mie”

“Vipi mbona Madam hatoki, au anaenda saa ngapi kazini?” Nikahoji huku nikipaka siagi kwenye kipande cha mkate.

“Huwa anaondoka asubuhi sana kwa lengo la kuwahi foleni” Akazungumza Mwalimu James huku akiramba midomo yake.

“Kumbe ameshaondoka?”

“Yule ni mtu wa utaratibu, mambo yake yapo kwenye mpangilio kama askari Polisi”

“Na Bi mdogo naye, au amekwenda shule?”

“Nani?” Mwalimu akahoji.

“Namaanisha….”

“Nipo hapa!” Sauti ya Sarah ilinikatisha maneno yangu na kugeuka kumtazama.

“Oooh habari za asubuhi Sarah” Nikamsalimia kwa upendo.

“Hapana mimi sio Sarah, niite mama. Mimi ni mama mwenye nyumba au umesahau hilo” Sarah alizungumza huku akimsogelea Mwalimu James na kumkumbatia kichwa halafu akampiga busu la utosini.

“Samahani Mama karibu chai” Nikazungumza kwa sauti ya unyenyekevu.

“Koma wewe usinizeeshe mtoto mwenzio!” Sarah akajibu kwa jazba.

“Acha ukorofi basi” Mwalimu James akaunguruma.

“Wewe binti usipokuwa makini, utaondoka humu ndani” alisema Sarah kwa nyodo huku akirembua vile vimacho vyake kama goroli.

“Samahani, naomba nikaendelee na kazi” Nikazungumza kwa sauti ya unyenyekevu huku nikivuta hatua kutaka kuondoka.

“Hebu njoo hapa! Ukaendelee na kazi inamaana umetuona vikarakosi hapa?” Sarah akazungumza kwa amri.

Ikabidi nisimame kidogo kumsikiliza yule bosi wangu. Ndio kwasababu hata mbwa wa bosi wako pia ni bosi wako.

“Mwache aende bwana!” Mwalimu James akaingilia kati kwa sauti ya kukoroma.

“Nenda sasa unasubiri nini?” Sarah akaniambia kwa ghadhabu.

Taratiibu mtoto wa kike nikanyoosha miguu na kuelekea jikoni kwa mwendo wa kunyubulika. Huko nyuma nafikiri walikoma wenyewe kwa makusudi niliyokuwa nikiwamwagia. Chezea Farida weye, Utavunja ndoa!

Niliingia jikoni na kujibanza kwenye kona ya mlango kusikiliza mazungumzo ya wapuuzi wale. Nilikuwa na hamu kubwa sana ya kuelewa kilichokuwa kinaendelea ndani mle.

“Macho kodo!” Nikasikia Sarah akimwambia mwalimu James ambaye alikuwa amekodoa macho kuniangalia nilipokuwa naondoka.

“Kwani macho yana pazia!” Mwalimu James akazungumza huku akipeleka kikombe cha chai mdomoni.

“Nyoo umefuraaahi kumiliki wake watatu kwenye nyumba moja” Sarah akazungumza maneno ambayo yalimfanya Mwalimu James kupaliwa ile chai aliyokunywa na kukohoa mfurulizo.

“Utaniua we mwanamke!” Alizungumza Mwalimu James huku akiendelea kukohoa.

“Ufe tu kwani una faida gani hapa duniani?”

“Sasa mimi kosa langu ni lipi hapa?”

“Unafikiri sijasikia ulivyokuwa unamtongoza?”

“Inamaana umemsahau Farida wewe? Kale kabinti sio karahisi kiasi hicho”

“Haya sema utanioa lini?”

“Nitakuoa tu, ngoja nijipange kwanza”

“Usitake kupoteza lengo, ole wako ufanye ushenzi! Wazazi wangu wanajua nipo shule” Sarah alizungumza maneno ambayo yalianza kunipa mwanga.

Kumbe wale mbuzi waliachishana shule na kuwekana unyumba. Mbaya zaidi wanamdanganya Madam kwa kujifanya ni ndugu, Firauni wakubwa!

Mwalimu James aliinuka na kukamata begi lake la vitabu. Akamtazama Sarah kwa tabasamu la matumaini.

“Baade basi mke wangu”

“Kwenda zako! Tena usirudi hapa!” Sarah alizungumza kwa jazba kumsindikiza Mwalimu James aliyekuwa anatoka ndani mle.

Nilivuta pumzi na kuzitoa kwa mkupuo. Nikaachia tabasamu la matumaini huku nikijiona mshindi kwa kufanikisha hatua ya kwanza. Sasa nikajipanga kwaajili ya hatua nyingine kama vile mwanajeshi vitani. 



*****

Baada ya Madam na Mwalimu James kuondoka tulibaki mimi na Sarah katika nyumba ile. Nakumbuka nilikuwa jikoni nikiendelea na shughuli zangu za maandalizi ya chakula cha mchana. Ghafla nikasikia mtu akijikohoza nyuma yangu. Niligeuka na kumuona Sarah amesimama pembezoni mwa mlango huku amekunja mikono yake kifuani.

“Ooh Mother houiuse huyo!” Nikazungumza huku nikitabsamu.

“Njaa bwana mtu unapika haviivi. Au unapika mawe?” Sarah alizungumza kwa nyodo.

“Namalizia Bosi wangu” Nikajibu kwa heshima.

“Farida naomba nikuulize kitu mwanangu” Akazungumza huku akisogea karibu na pale nilipo.

“Nakusikiliza Mother house” Nikajibu huku nikimgeukia vizuri.

“Ikitokea Mwalimes akaendelea kukutaka utachukua maamuzi gani?” Sarah alizhoji kwa umakini mkubwa.

“Mnh!” Nikaguna na kujikuta nikikosa jibu la haraka.

“Unaguna nini sasa?”

“Sijafahamu nitafanya nini kwasababu sijaona dalili yoyote ya jambo kama hilo” Nikaeleza.

“Sina maana mbaya mdogo wangu, naomba usinihofie kabisa”

“Sarah nafikiri unanifahamu vizuri”

“Kama unampenda kwa dhati Mwalimu James mimi nitakuachia kwasababu najua hata yeye anakupenda kuliko hata anavyonipenda mimi” Sarah akaeleza.

Yale maneno Ya Sarah nikaona yakinichefua tu, Sikutoa jibu lolote na wala sikutaka kuendelea kujadiliana naye jambo kama lile. Niligeuka na kuendelea na shughuli zangu.

“Kusema ukweli binafsi sina mapenzi a dhati na huyo Mwalimu James” Sarah alizungumza kwa sauti ya taratibu kama vile anajilazimisha.

“Nipo hapa kwaajili ya kusukuma siku tu. Muda wa masomo ukiisha najiondokea” Sarah akazungumza na kunifanya nigeuke kumtazama kwa makini. Nikahisi kitu kipya kilikuwa kinaendelea ndani ya nyumba ile ya maigizo.

“Usinitumbulie macho. Kama ulikuwa hujui ndio ulijue hilo” Akasisitiza.

“Inamaana wazazi wako wanajua upo shule?”

“Na kama wangeujua ukweli nafikiri wangeshanitoa roho” Sarah akasema.

“Kwanini sasa unafanya hivo Sarah?” Nikahoji kwa uchungu mkubwa sana.

“Kwasababu Sipendi shule!”

“Lakini shule ina umuhimu sana katika maisha yako Sarah”

“Kama shule ingekuwa na umuhimu basi hata wewe usingeikimbia na kuvamia shughuli za kitumwa” Sarah akazungumza.

“Napambana, najua ipo siku nitarudi shule na kuendelea na masomo” Nikazungumza kwa uchungu mkubwa.

Maneno yangu yalimfanya Sarah kuangua kicheko kwa sauti. Alicheka sana kiasi cha kupaliwa na mate akawa anakohoa mfurulizo.

“Sikiliza Farida nikwambie kitu mpenzi” Alizungumza Sarah na kukohoa tena mara mbili

Nikageuza macho yangu na kumtazama kwa makini kuweza kusikia alichokuwa amekusudia kunieleza.

“Unajua mzee anakupenda sanaaa”

“Mzee gani?” nikahoji kwa umakini.

“Mzee baba, father house au Baba mwenye nyumba. Ninamaanisha Mwalimu James” Sarah akazungumza kwa msisitizo.

“Kwahiyo unataka kusemaje?”

“Kama nilivyokwambia mimi sina mapenzi ya dhati kwa yule mwanaume” Sarah akazungumza.

“Hata mimi nalijua hilo. Madam pekee ndio mwenye mapenzi ya dhati kwa mume wake” Nikasema.

“Hebu usinitajie hicho kituko nisije nikatapika”

“Yaani unamwita Madam kituko?” Nikahoji kwa mshangao.

“Kwani wewe unamuona yupo sawa yule. Kama angekuwa sawa asingekubali kuishi na mke mwenzie nyumba moja halafu asijue kinachoendelea” Sarah akazungumza kwa kebehi.

“Sasa kwanini unataka kuharibu ndoa ya watu?” Nikahoji kwa umakini.

“Tamaa zao ndizo zinawaponza, hapa nipo kazini” Sarah akazungumza kwa sauti ndogo lakini iliyokuwa imejaa misisitizo.

“Inamaana na wewe umekuja hapa kama mfanya kazi?” Nikahoi baada ya kuhisi maelezo yake yalikuwa yananichanganya kadri muda ulivyokuwa unasonga.

“Pesa mama, nipo hapa natafuta pesa. Nikifanikiwa tu nayeyuka kama barafu” Sarah akazungumza kwa kujiamini huku akionesha msisitizo kwa macho.

“Kumbe unalipwa kama mfanyakazi?” Nikazidi kuchanganywa na taarifa zake.

“Mimi sio mfanyakazi best. Madam anajua mimi ni ndugu wa mume wake. Na Mwalimu James anadhani mimi ni mke wake.” Sarah akaeleza.

“Sasa ukweli ni upi hapo?”

“Kila mmoja anajidanganya”

“Ndio unipe sasa huo ukweli” Nikasisitiza. 



“Ndio unipe sasa huo ukweli” Nikasisitiza.

“Ukweli mimi ni mwizi” Sarah akasema kwa ufupi.

“Hata mimi ninajua wewe ni mwizi unaiba mume wa mtu”

“Hapana, mimi sio mwizi wa mapenzi bali ni mwizi wa mali za Madam. Nataka kuhakikisha nawakausha kabisa na kuwaacha kama walivyozaliwa” Sarah alizunguma kwa msisitizo.

“Mnh kwanini unanieleza yote hayo?” Nikahoji kwa mashaka.

“Kwasababu nataka kushirikiana na wewe! Tukifanikiwa tutauonesha ulimwengu kuwa shule sio lazima” Sarah akazunguma kwa msisitizo na kujiamini.

“Niondolee upuzi wako hapa! Sijawahi na sitathubutu kujiingiza kwenye dhambi kama hiyo” Nikazungumza kwa msisitizo wa hali ya juu.

“Nakujua vizuri mama wa misimamo, lakini kwanza unatakiwa kukumbuka jinsi Mwalimu James alivosababisha ufukuzwe shule” Sarah alizunguma maneno ambayo kusema kweli yaliniingia sana na kuhisi kutamani kuungana na binti yule katika mikakati yake. Lakini nilipokumbuka wema wa Madam Manka nikajikuta napoteza matumaini kabisa.

“Hapana Mama naomba uendelee na mipango yako peke yako” Nikazungumza kwa tahadhari.

“Labda nikuondoe wasiwasi, katika mpango huu sipo pekeyangu” Sarah akaeleza.

Nikageuza macho na kumtazama kwa makini kutaka kusikia mshirika mwenzie ni nani.

“Nashirikiana na mpenzi wangu” Sarah akasema.

“We si umesema Mwalimu James hafahamu mpango wako?”

“Nimekwambia mpenzi wangu sio mwalimu James” Sarah akasisitiza na kuendelea kuniweka katika wakati mgumu.

“Inamaana una mwanaume mwengine?” Nikahoji kwa umakini.

“Huyo ndiye ninayempenda na yeye ananipenda sana. Ni yeye aliyenishauri niache shule na kujiingiza katika mpango huu” Sarah akaeleza.

“Mungu wangu we Sarah! Kwanini unafanya mambo ya kipuuzi kiasi hicho?” Nikahoji kwa msisitizo.

“Kwasababu ya Mapenzi, Nampenda sana Mwanaume wangu. Najua baada ya kukamilisha mipango yetu, mimi na yeye tutafunga ndoa na kuishi kama malaika” Sarah akazungumza kwa hisia huku ameweka kiganja cha mkono kifuani.

“Malaika waliolaaniwa” Nikasema kwa jazba.

“Kwahiyo unasemaje upo tayari nikupe mchongo mzima?”

“Naomba uondoke Sarah, niko bize” Nikazungumza kwa msisitzio.

“Utasugua sufuria hadi kucha ziote sugu hizo. Na huyo Madam wako akishafirisika sijui utahamia wapi” Sarah akaunguma kwa kebehi.

Niliinua macho yangu na kumtazama binti yule kwa macho ya hudhuni na kuachia tabasamu la masikitiko. Sauti ya mlango uliokuwa ukigongwa ilitufanya tuhamishe akili zetu na kusikiliza kwa makini. Sarah akainua mkono na kusoma saa iliyokuwa mkononi mwake.

“Muda ndio huu Stelling amefika” Sarah akazungumza na kuondoka jikoni mle akiniacha katika mshangao wa hali ya juu.

Nilivuta pumzi na kuziachia kwa mkupuo huku nikihisi kuchanganyikiwa kutokana na kufahamu mpango wa Sarah ndani ya nyumba ile. Kwakuwa nilikuwa namfahamu vizuri binti yule, hivyo niliamini kabisa maneno aliyokuwa yanamtoka kinywani mwake.

“Lazima niokoe ndoa ya Madam, tena haraka sana” Nikajikuta nikizungumza kwa sauti ndogo lakini iliyokuwa imejaa msisitizo.

“Faridaaaa!” Niligutushwa na sauti ya Sarah iliokuwa ikiniita kutokea sebleni. Nikameza funda la mate kwanza na kuachia pumzi ndefu.

“Farida mpenziii” Sauti ya Sarah ikaita tena.

“Abee”

“Njoo mpendwa” Sarah alizungumza.

Nilikausha mikono yangu kwa kitambaa kisha nikavuta hatua kuelekea sebleni. Nilipotokeza tu sura yangu sebleni pale nikakutana uso kwa uso na mgeni yule.

“Mungu wangu! Huyu kiumbe anafanya nini hapa?” nikazungumza mwenyewe huku nikihisi mapigo ya moyo yakinienda mbio.

Mgeni naye alionekana kushituka baada ya kuniona. Ni wazi kabisa hakutegemea kunikuta katika mazingira kama yale. Akabaki mdomo wazi huku akijibaraguza asishitukiwe na Sarah. 



“Vipi msosi tayari?” Sarah akahoji.

“Namalizia kupika…” Nikazungumza kwa sauti ya kuogofya.

“Kutana na Dullah, huyu ndio Daktari wangu wa Mapenzi. Ndio yule mwanaume niliyekwambia kuwa tunapendana sana” Sarah alizungumza kwa kujidai.

Ndugu msomaji Dullah huyo niliyekuwa nikitambulishwa na Sarah alikuwa ni yule Dullah wa dada Halima. Ni yule Dullah aliyekutana kimapenzi na Sakina kwenye jiko la mgahawa wa mama Halima. Ndiye yule Dullah aliyewahi kunitongoza na kupelekea nikagombana na Sakina. Huyo Dullah wa siku hiyo ndiye huyohuyo Dullah unayemfahamu wewe ndugu msomaji.

“Nashukuru kumfahamu, Karibu sana Dullah” Nilikazungumza kwa sauti ndogo ya upendo na iliyokuwa imejaa heshima.

“Yeye ni mwenyeji anapaswa kukukaribisha wewe” Sarah alizungumza kwa utani na kutufanya tutoe vicheko vya kinafki.


ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

BLOG