Search This Blog

Sunday, April 18, 2021

KITUMBUA CHA KIHINDI - 2

   


Chombezo : Kitumbua Cha Kihindi

Sehemu Ya Pili (2)


“Mama unafanya nini hapa!” macho yalimtoka Magosho na kuhoji kwa mshangao.

“Mume yangu iko piga mimi. Kama iko kuje ambie mimi hapana fika hapa?” alisema Bi.Fahreen huku akiingia kwenye kabati la nguo chafu za Magosho. Aliamini kuwa mlango uliokuwa ukifunguliwa ulikuwa ni wa chumbani kwao na Mr.Nakeshiwar alikuwa anamtafuta baada ya kuto muona chumbani.

Magosho akawa katika mshangao mkubwa kutokana na kile kilichokuwa kikitokea chumbani kwake. Akatulia ili kuona ni kitu gani ambacho kilikuwa kinaendelea. Lakini muda ukapita pasipo kuona chochote. Bi.Fahreen naye alipoona kulikuwa kumetulia akatoka kule kabatini.

“Siku mema toto zuri” Bi.fahreen alisema na kutoka mle chumbani kwa Magosho huku akitetemeka kwa woga. Akanyanta hadi kwenye mlango wa chumbani kwao na kusimama kwa sekunde kadhaa kusikilizia. Alipoona kimya akaushika mlango na kuingia. Alimkuta mume wake amelala akiendelea na zoezi lake la kukoroma mithili ya mashine na kukobolea nafaka. Bi.Fahreen baada ya kufunga mlango alifanikiwa kupanda kitandani pasipo kugundulika. Alimsogelea zaidi mume wake na kumkumbatia ili kuicha dhambi aliyokuwa ametaka kuitenda.

****

Siku zilisogea na kusonga huku mawazo yakiwa yanamsonga Bi.Fahreen juu ya penzi la kijana Magosho. Siku zilivyozidi kusonga mbele ndivyo mwanamke yule wa kihindi alivyojiona akizidi kuchanganyikiwa na kijana yule.

Akiwa amejilaza kitandani huku mto ukiwa kifuani pake ameubana kwa nguvu alijikuta akiubusu mara kadhaa mto ule.

“Lazima pate ile toto zuri leo” Bi.Fahreen alijikuta akizungumza kwa sauti. Akapaza sauti na kumuita Magosho ambaye alikuwa jikoni akifanya usafi.

Magosho aliposikia sauti ya mke wa bosi wake aliwacha kazi na kumfuata. Alipofika kwenye mlango wa chumbani akasimama na kugonga taratibu na kwa unyenyekevu mkubwa. Sauti iliyotokea chumbani ilimruhusu aingie. Magosho akasita na kutamani kugoma kuingia lakini kwakuwa alikuwa ni mke wa bosi wake akaona angeonekana mjeuri. Kwa tahadhari kubwa alishika kitasa cha mlango ule na kusukuma mlango taratibu huku akiwa na wasiwasi moyoni mwake kama vile kibaka.

Magosho alimkuta Bi.Fahreen akiwa amejitandaza kitandani huku amejifunga kanga moja tu kifuani. Magosho akataka kurudi lakini akashituliwa na sauti ya mama yule.

“Hapana gopa bhanaaa, veve kuje tu” alisema Bi.Fahreen huku akijiinua kutoka pale kwenye kitanda.

Mwanamke yule akajifanya kulikuwa na kitu anakwenda kuchukuwa kwenye kabati. Magosho akawa ametumbua macho kumuangalia mama yule jinsi ambavyo alikuwa akichezesha kwa makusudi ule mzigo wake aliobarikiwa na mola.

Bi.Fahreen alikuwa akijitambua kuwa alikuwa amebarikiwa. Si kweli kwamba kulikuwa na kitu alichotaka kukichukua kwenye kabati, bali alikuwa akijitembelesha makusudi tu ili kumuonesha Magosho kwamba yaliyomo yalikuwemo kweli na wala hayakuwa yale ya mito na magodoro.

Weupe wa ngozi ya mama yule ulizidi kung’aa ndani ya ile kanga aliyokuwa amejifunga kifuani na kupelekea miguu yake iliyokuwa imejazia vizuri kuonekana na mvuto mara mbili zaidi. Vijana wanasema mguu wa bia sijui mguu wa nini, Mnh! Haya bwana mie sijui. Magosho aliweza kubaini urembo wa mama yule ambaye alikuwa ameshawahiwa na kumilikiwa na Bwana Nakeshiwar.

“Duh! Utadhani hakuwahi kuzaa!” alijisemea Magosho huku akiendelea kumtumbulia macho na kumthaminisha mama yule wa kihindi aliyekuwa akijitembelesha mbele ya macho yake kwa uchokozi kabisa.

Bi.Fahreen alipofika pale kabatini akajifanya kupekuwa pekuwa sehemu ya juu ya kabati. Kitendo kile cha kupekuapekua kilipelekea lile zigo lake kutikisika na kutetema kila alipokuwa akijitingisha. Magosho akajikuta akizidi kutoa macho kwa mshangao kijana wawatu na kusahau kabisa kama ile ilikuwa ni mali ya mwenyewe Mr. Nakeshiwar. Yani kama ungepata fursa ya kumuona kijana yule ungesema alikuwa ameona muujiza wa mazingaombwe.

“Mnh! unaweza ukajikuta unatolewa roho na Nakeshiwar hivi hivi haki ya mungu!” Magosho akajisemea kimoyo moyo huku akihisi jogoo aliyekuwa amefungiwa bandani akiwika. Akapeleka mkono wake haraka sana na kumdaka koo kisha akambana kwa kamba ya lastiki.

“Haya furukuta sasa” akamuambia jogoo wake kwa sauti ya chini kama vile alikuwa akizungumza na binadamu mwenzake.

Bi.Fahreen akageuka na kushika kiuno huku akipumua kwa nguvu kama vile kitu alichokuwa akikitafuta alikuwa amekikosa. Magosho akainamisha macho chini kujifanya hakuwa akimuangalia mwanamke yule alipokuwa akileta mafindofindo pale kwenye kabati.

“Gosoo” aliita Bi.Fahreen.

“Naam mama” Magosho aliitika na kujianya kushituka kama vile kulikuwa na kitu mbalisana anakiwaza.

“Mimi taka kupa veve kazi sawa?” Alizungumza Bi. Fahreen kwa

“Sawa mama” Magosho alijibu na kukwepesha macho kutoka kwa Bi.Fahreen ambaye alikuwa akimtazama kwa jicho lililokuwa limechoka kuangalia.

Bi.Fahreen akakatiza mbele ya Magosho na kwenda kwenye kitanda, alipiga magoti kisha akainamisha kichwa kuchungulia chini ya uvungu.

“Mama weeee!” Magosho alijikuta akihamaki huku ameweka mikono yake kinywani baada ya mama yule wa kihindi kuinama na kumuachia ule mzigo wake ukiwa umebinuka juu utafikiri breki ya katapila. Bi.Fahreen kama ilivyo kawaida yake, kule chini ya uvungu nako akawa anajitingisha na kufanya zigo kuelemea na kuwa kama vile likitaka kudondoka.

“Dah! Kwa kweli Nakeshiwar anafaidi” alisema Magosho kimoyo moyo huku akibana mapaja yake kwa nguvu angalau apate ahuweni kutokana na hali aliyokuwa akiisikia. Baada ya kuona kubana miguu hakumsaidii akapeleka mikono na kujiminya kwa nguvu maeneo ya Pwani ya Afrika Mashariki.

“Bahati yake ni mke wa Bosi, vinginevyo leo ingefahamika” Magosho alijisemea huku akimeza funda la mate.

Bi.Fahreen alitoka kule chini ya uvungu bila kitu chochote. Magosho alikuwa na hamu kubwa ya kutaka kukiona hicho alichokuwa akikitafuta mke wa bosi wake. Bi.Fahreen akasimama na kushika tena kiuno chake kuashiria kuwa alikuwa amechoka kutafuta kitu ambacho alikuwa hakioni. Akamtazama Magosho ambaye alikuwa amesimama huku mguu mmoja akiwa ameupitisha mbele ya mguu mwingine ili kuficha mke wa bosi wake asibaini kama alikuwa ameharibikiwa.

“Sasa veve Goso iko simama tuu, hapana choka veve?” alihoji Bi.Fahreen.

“Basi mama ngoja mimi niende, halafu utaniita” alisema Magosho huku akipepesa macho kukwepa kuangaliana na mwanamke yule.

“No! kuje kae hapa kwa tanda yangu” alisema Bi.Fahreen.

Jamani jamani nyie duniani hapa kuna mambo! Sasa Magosho wawatu vilealivyokuwa ameharibikiwa halafu aende akaketi kitandani, ndugu msomaji mbona kama sielewi hivi kwa upande wangu Mnh! Kuna mtego na tego, sasa lile naona lilikuwa nit ego.

“Hapana mama, ngoja nikae hapa kwenye kochi” alisema Magosho na kuelekea kuketi kwenye kochi lililokuwemo mle chumbani.

Bi.Fahreen akamtupia tabasamu la mahaba lililokuwa limepambwa vyema kwa lipsi zake pana zilizokuwa na wekundu wa asili.

Mwanamke yule wa kihindi alirudi tena kabatini na kufungua mlango wa chini. Safari hii alitoa nguo kutoka kabatini na kwenda kuzirusha pale kwenye kochi alipokuwa ameketi Magosho. Jamani watu wengine wana vituko! Magosho alipoangalia vizuri nguo zile akabaini kuwa zilikuwa ni nguo za ndani tupu za mama yule. Kichwani akajawa na mshangao na maswali ambayo majibu yake hayakuweza kupatikana kwa wakati ule.

“Inamaana leo napewa nguo za ndani kufua? Hii sasa kali!” Magosho alijisemea kimoyo moyo huku akizitupia jicho la wizi nguo zile.

Bi.Fahreen akamsogele taratiibu huku akirembua yale macho yake. Safari hii alizidisha vituko kwa kijana wa watu ambaye alikuwa amemvumilia kwa muda mrefu. Alipeleka mikono yake na kumshika mabegani. Alitulia kwa sekunde kadhaa akimtazama usoni pasipo kuzungumza neon lolote. Magosho akawa akihangaika kuangalia pembeni kukwepa macho ya mama yule aliyekuwa akimletea mauzauza.

Bi.fahreen akainua mguu wake wa kushoto na kuuweka juu ya mapaja ya Magosho huku akiendelea kumtazama usoni mtoto wa mwanamke mwenzie. Magosho aligutuka baada ya kitendo kile alichofanyiwa na mke wa bosi wake.

“Mama!” alihamaki Magosho.

“Shiii! Mimi taka kupe kazi veve, iko situka nini sasa?” alihoji Bi.Fahreen huku viganja vya mikono yake vikipita pita kwenye shingo ya Magosho ambaye alikuwa ametulia baada ya kunyamazishwa na mama yule.

“Taka veve fua nguo hizo halafu kuje panga kwa kabati. Sawa?” alisema Bi.Fahreen huku ule mguu wake mmoja ukiwa bado kwenye mapaja ya Magosho. Kitendo cha kupandisha ule mguu wake pale kilipelekea ile khanga aliyokuwa amevaa kufunuka upande mmoja na kuzidi kuonesha sehemu kubwa ya mwili wake ambayo haikupaswa kuonekana na Magosho ama mtu mwingine yeyote zaidi na Mr. Nakeshiwar pekee.

Magosho alijikuta akitetemeka kutokana na vitendo vya mama yule mwenye asili ya kihindi. Bi.Fahreen akapeleka mkono wake na kufanikiwa kuzidaka zana zilizokuwa zimefichwa barabara. Magosho akashituka na kujikuta akizidi kutetemeka.

“Lakini mama…!” Magosho alizungumza kwa sauti iliyokuwa ikikwama kwama.

“Nini bhanaaa?...mimi taka onesa kitu veve” alizungumza Bi.Fahreen kwa sauti iliyotokea puani na kuzidi kumchanganya Magosho wawatu kaka wa Ashura.

Kiukweli Magosho alikuwa amepatikana mtoto wa watu wa marehemu mama Ashura. Kama ni ndege basi tungesema alikuwa ameingia mwenyewe kwenye tundu alilokuwa ametegewa na kilichobakia kilikuwa ni kuchinjwa tu na kuliwa.

Sauti ya viatu vya Mr. Nakeshiwar ilisikika ikigonga sakafu ya sebule ya nyumba ile. Bi.Fahreen pamoja na Magosho wakajikuta wakishituka baada ya kusikia vishindo vile. Walikuwa wamechanganyikiwa wasijue cha kufanya. Ilikuwa ni vigumu kwa mtu kutoka pasipo kuonekana. Hivyo walikuwa hawajui wafanye nini ili Mr. Nakeshiwar asiweze kumuona Magosho mle chumbani kwake.

“Naingia huku chooni” alisema Magosho huku akionekana kuchanganyikiwa.

“No! yeye penda ingia humo, kama iko toka kazini” alisema Bi.Fahreen huku akijaribu kuzunguusha macho kutafuta mahali ambapo angemficha Magosho. Mazingira ya chumbani mle ilikuwa ni vigumu kumficha mtu asionekane.

Vishindo vilikuwa vikikaribia kwa haraka kwenye mlango wa chumba kile. Vilipofika mlangoni kitasa cha mlango ule kilishikwa. Pasipo kusubiri chochote Magosho akaingia chooni kujificha ingawa aliambiwa kuwa Mr. yule huwa kila alipokuwa akitoka kazini alipendelea kuingia chooni. Mlango ulifunguliwa na Mr. Nakeshiwar akaingia.

Lilikuwa ni jambo la kuchekesha kama sio kusikitisha. Bi.Fahreen alishindwa kuficha wasiwasi wake kwa mume wake. Alikuwa akitetemeka utafikiri dereva wa trekta. Mr. Nakeshiwar akamtazama kwa jicho la tatu ili kuweza kubaini tatizo alilokuwa nalo mke wake.

“Vipi iko shida yoyote Fahreen?” alihoji Mr. Nakeshiwar

“No problem Darling. Kwanini today iko narudi mapema, any problem?” alihoji Bi.Fahreen huku akijibaraguza kukunja zile nguo zake zilizokuwa kwenye kochi.

“I come for my files” (Nimefuata mafaili yangu) alisema Nakeshiwar huku akifungua droo ya kitanda na kupekua pekua. Baada ya sekunde kadhaa alionekana kuyapata na kuyatoa. Aliyaweka kitandani kisha akausogelea mlango wa chooni kama ilivyokuwa kawaida yake.

Bi.Fahreen akajikuta akiishiwa nguvu na kulegea huku akishindwa kujizuia kutetemeka. Nakeshiwar alishika kitasa cha mlango wa chooni na kumgeukia mke wake.

“Leo iko problem” alisema Nakeshiwar akiwa amesimama sawa na mlango.

Kule chooni Magosho alijikuta akijikojolea kwa kitete alichokuwa nacho. Alisikia jinsi kitasa cha mlango ule wa chooni kilivyokamatwa barabara na Mr. Nakeshiwar. Akajikuta akiijutia nafsi yake kwa kukubali kuingia chumbani mle.

“Masikini mimi ninahukumiwa bila hatia” alijisemea Magosho huku akiwa amejikunyata kwenye pembe ya choo kile kilichokuwa kidogo kiasi cha kukosa pa kujificha.

Magosho alikuwa akimhurumia sana mdogo wake Ashura ambaye angebakia mpweke baada ya kifo chake ambacho kingemkuta muda mfupi uliofuata baada ya kutiwa mikononi na baba yule wa kihindi.

Ghafla kitasa cha mlango ule kilinyongwa na mlango ukaanza kusukumwa ndani taratiibu. Masikini Kijana Maosho akahisi haja kubwa na ndoo zikikaribia kumtoka kwa pamoja. Ndugu msomaji nisikufiche, naandika hadi nahisi kutetemeka mwenyewe kwa tukio hili. Mnh! Mbona kasheshe.




Mr. Nakeshwar alipokuwa akisukuma mlango simu yake ya mkononi iliita. Aliipokea na kuanza kuongea na mtu aliyempigia huku akiwa amesimama kwenye mlango wa choo ambao ulikuwa wazi. Aliuwachia ghafla mlango ule na kurudi kitandani ambako alichukua mafaili yake na kuyaweka kwenye bahasha kisha akamgeukia mke wake.

“Najua kuna kasoro. Lakini niache niende sitachelewa kurudi” alisema Nakeshiwar na kutoka kwa kasi ya ajabu mle chumbani. Inawezekana simu aliyopigiwa ndiyo iliyomfanya kuwa na haraka kiasi kile.

Magosho akiwa nyuma ya mlango wa choo hakufahamu kilichokuwa kinaendelea huko nje. Alikuwa amesimama sawasawa na ukuta huku akiwa amefumba macho. Bi.Fahreen alimfuata nyuma mume wake na kuhakikisha kuwa alipanda gari na kuondoka. Alirejea chumbani kwake na kufungua mlango wa chooni. Alimtoa Magosho haraka sana kisha akaenda kujitupa kitandani. Hakuamini kama alikuwa amepona kuachika ama kuuliwa na jamaa yule wa kihindi.

Magosho alijikuta miguu ikigongana na kushindwa kutembea. Hakuweza kuelewa ni kwa namna gani aliweza kutoka chumbani mle akiwa salama. Mawazo yake aliamini kuwa ndani ya nyumba ile angetolewa kwa machela tena akiwa maiti. Akaapa kuwa hatothubutu kumkaribia tena Bi.Fahreen.

* * *

Ashura aliendelea kufanya biashara vizuri kutokana na mtaji aliopewa na kaka yake mpendwa Magosho. Mtaji wake wa kuchoma vitumbua ulikuwa kiasi cha kumuwezesha kufungua saluni ndogo ya wanawake. Pamoja na kwamba saluni ilikuwa ikimuingizia pesa kwa kiasi kikubwa lakini biashara yake ya kukaanga mihogo na kuchoma vitumbua hakuiwacha. Aliweza kufanya vyote hivyo kwa wakati mmoja. Asubuhi alijikita katika kuchoma vitumbua na mchana alikwenda saluni.

Kadri siku zilivyokuwa zikisonga mbele ndivyo akili ya Ashura ilivyokuwa ikikomaa kibiashara. Malengo yake yalikuwa ni kukua zaidi na kuwa miongoniwa wafanya biashara wakubwa sana jijini Dar. Hivyo wakati wote alikuwa akiumiza kichwa chake kuona ni mbinu gani atumie katika kukua kwake kibiashara.

Pesa ambazo alizikusanya kwenye kupika vitumbua na nyingine alizopewa na kaka yake mpendwa alichanganya na pesa zilizopatikana saluni kisha alizipeleka dukani kununulia vifaa vya saluni. Kitendo kile kilipelekea Ashura kubakiwa na pesa za mtaji wa vitumbua tu tena zilikuwa ni za mtaji mdogo sana. Aliamini mtaji wake ungeweza kurejea katika hali yake ya kawaida punde saluni ile itakapoanza kumuingizia pesa kwa kasi kutokana na zana mpya ambazo aliziongeza.

Siku moja akiwa kwenye biashara yake ya vitumbua alifika mteja mmoja aliyekuwa anahitaji vitumbua.

“Hivi Ashura ni kweli au unajichetua tu?” mteja yule alizungumza wakati Ashura alipokuwa akimfungia vitumbua mteja wake.

“Kwanini mteja wangu?” alihoji Ashura huku akiendelea kumfungia mteja wake.

“Mnh una moyo shoga” mteja yule alizungumza huku akipokea vitumbua vyake kutoka kwa Ashura.

“Mbona sikuelewi jamani”

“Leo umefika saluni kwako?”

“Hapana, namalizia hapa niende kufungua”

“Mnh, kweli hujui kitu?” alihoji mwanamke yule.

“Mbona sikuelewishoga, kwani kuna nini?” alihoji Ashura huku akimtazama kwa makini mteja yule.

“Mnh umbea huu nao” mwanamke yule akajisemesha.

“Hebu niambie bwana ni kitu gani kinaendelea” Ashura alianza kupatwa na mashaka kutokana na maneno ya yule mteja wake.

“Shoga umeumia, kama kweli haufahamu basi hiyo ndio taarifa” alizungumza mwanamke yule na kuanza kundka.

“Wewe hebu subiri kwanza” Ashura alijaribu kumuita mwanamke yule ili ampatie maelezo ya kueleweka.

Nakwambia mwanamke yule alikuwa kama vile ametumwa kwenda kumwaga umbea na kuondoka. Pamoja na kwamba Ashura alipaza sauti kumuita lakini hakugeuka nyuma wala kuongeza neno lolote. Alikuwa akitembea huku akijitikisa kishankupe na kamkono kake akikachezesha utafikiri kalikuwa kanadondoka.

Ashura alifunga haraka haraka biashara yake na kuita boda kuelekea huko saluni ambako Shankupe yule alikuw amejaribu kumpatia taarifa zilizokuwa hazieleweki.

Ndugu msomaji huwezi kuamini alichokikuta huko saluni kwake binti yule aliyekuwa mchakarikaji katika kusaka mshiko. Saluni ilikuwa imevunjwa na vibaka kisha vifaa vyote vilikuwa vimeibwa. Ama kweli ng’ombe wa masikini hazai, na wa moja havai mbili.

Alishindwa kujizuia kutoa machozi na kulia kwa kwikwi kutokana na uchungu uliokuwa ukifukuta ndani ya kifua chake. Aliinua macho yake na kuangalia mawinguni huku akisikitika kama vile anatupa lawama kwa Mungu kutokana na kile kilichokuwa kimemtokea.

“Kwanini mimi Mungu wangu! Kwanini kila siku ni mimi tu na kaka yangu?” alizungumza kwa uchungu Ashura huku akiendelea kumiminika machozi kwenye mashavu yake.

Hata kama angelia hadi kupasuka unadhani ingesaidia nini? Akajikokota kwa taabu kujirudisha nyumbani huku akihisi mzigo mkubwa sana wa dunia ulikuwa kichwani mwake.

Mtaji ule wa saluni ulipatikana kwa mbinde tena kwa muda mrefu sana. Kutokana na sababu ile ingewachukua muda mwingine mrefu sana kukusanya pesa kwaajili ya kufungua tena saluni. Kwa kifupi Ashura aliamua kukata tamaa ya kufanya biashara ya saluni pamoja na kwamba ndiyo aliyokuwa akiitegemea kama njia kuu ya kumtoa kimaisha yeye pamoja na kaka yake Magosho.

****

Taarifa za kuvunjwa kwa saluni ya Ashura na kuibiwa ilimfikia Magosho na kumfanya kuwa na simanzi wakati wote. Alimhurumia sana mdogo wake, hakupenda kumuona akipata taabu ama kuwa ni mtu mwenye hudhuni. Alifahamu wazi kuwa tukio lile lilikuwa limemuumiza sana mdogo wake kipenzi Ashura.

Akiwa amekaa kwenye jiwe moja kubwa lililopo nje ya nyumba ya Mr. Nakeshiwar akiendelea kuwaza na kuwazua namna ya kujikwamua kimaisha yeye na mdogo wake. Mambo yote yaliyokuwa yakimtokea aliyaona kama vile alikuwa ni chukizo kwa Mungu. Kama kweli Mungu ndiye mpangaji wa kila jambo, ni kwanini ameamua kuipangia familia yake matatizo kiasi kile. Hata hivyo hakuwa na namna kwasababu hata yule aliyekuwa anamlaumu hakuwa anampa maelezo wala majibu yoyote. Akavuta pumzi na kuziruhusu kutoka nje kwa kuzisukuma kwa nguvu. Alitamani kupata pesa za haraka ili kurudisha mtaji wa dada yake na kurejesha Amani ya moyo wa ndugu yake huyo. Lakini angezipata wapi hizo pesa? Mshahara ambao alikuwa akipewa ulikuwa hautoshi ingawa uliongezwa mara mbili na yule mwanamke wa kihindi.

Bi.Fahreen ambaye alikuwa ndani akatoka huku kiunoni mwake akiwa amejifunga Kitambaa kirefu kilichofika hadi chini na juu alivalia kiblauzi kifupi ambacho kiliacha wazi tumbo lake. Na begani alikuwa ameweka mtandio uliokuwa wa kitambaa laini. Kwa ufupi ni kwamba alikuwa amevalia kiasili, yaani kihindi. Alipomuona Magosho amejiinamia mama yule akamsogelea taratibu na kwenda kuchutama mbele yake.

“Vipi Goso, iko problem?” alihoji Bi.Fahreen kwa sauti iliyo jaa huruma na upendo.

“Hapana mama” Magosho alijibu kwa mshituko kidogo kwasababu hakuwa ametegemea kupokea swali kutoka kwa mtu yoyote yule hasa kwa wakati ule.

“Hapana wakati iko najiinamia kama jingajinga” alizungumza mama yule kwa msisitizo.

“Ndio mama nina tatizo”alijibu Magosho kwa unyonge pasipo kumtazama Mwanamke yule usoni.

“Mimi weza saidia veve?” alihoji Bi.Fahreen kwa umakini mkubwa.

Magosho akawa kimya akitafakari lile swali la Bi.Fahreen. Aliamini kabisa alikuwa na uwezo wa kumsaidia. Lakini hakupenda kutoa matatizo ambayo yalikuwa yakimkabili ndani ya familia yake. Siku zote alipendelea kujaribu kwanza kupambana na changamoto na kama angeshindwa basi angemwambia mtu mwingine hasa kama kungekuwa na ulazima.

Sababu nyingine iliyokuwa ikimpa kigugumizi Magosho ni kwamba alikwisha zifahamu tabia za mama yule wa kihindi ambazo hakuwa anazipenda. Alikuwa akijitahidi kujiweka mbali naye ili asije kumletea balaa kutoka kwa mume wake. Hivyo aliamini kama angemueleza suala lile, lingekuwa ni sababu tosha ya kuwaweka karibu jambo ambalo hakutaka hata kulisikia. Aliinua macho na kumjibu.

“Hapana mama. Hakuna tatizo”

“Veve si iko sema iko problem?”

“Mwili tu umechoka, lakini naamini utakuwa vizuri punde” Magosho akajibaraguza.

“Pole sana Goso. Mimi taka veve sindikize mimi” alisema Bi.Fahreen.

“Wapi mama!” Magosho alihoji kwa kuhamaki.

“No swali! Sema sindikize mimi”

“Lakini mama, nilikuwa nataka kuandaa chakula cha mtoto” Magosho alijaribu ili kuweka vikwazo makusudi vya kutoka na mwanamke yule.

“Nakuwa jeuri sio?”

“Hapana mama”

“Nabisana na mimi?”

“Hapana mama, nilikuwa nasema tu?”

“Bosi yako iko ndani nalala, nataka veve sindikize mimi. Kama iko kataa sema”

“Sawa mama twende” alijibu Magosho huku akijiinua kutoka pale kwenye jiwe. Ilibidi akubali tu kwasababu kama angekataa kufanya vile, yule mwanamke angekwenda kushitaki kwa mume wake na kumletea shida Magosho. Hivyo hakupenda kuongeza matatizo juu ya matatizo mengine.

Walikwenda kuchukua gari ya Mr. Nakeshiwar na kuondoka nayo ikiendeshwa na Bi.Fahreen. Mazingira ambayo gari ile ilipokuwa ikielekea hayakuwa mageni sana kwa Magosho. Siku moja alikwisha fika akiwa na mke wa bosi wake yule yule Bi.Fahreen. Kumbukumbu za matukio yaliyomtokea siku ile zikamjia. Kule ndiko siku hiyo Bi.Fahreen aliyokuwa amezidiwa na kulegea kutokana na ugonjwa wa ajabu. Gari ile ilikwenda kusimama mahali pale pale ambapo ilisimama siku walipofika kwa mara ya kwanza. Bi.Fahreen akamgeukia Magosho na kumtazama kidogo kisha akanyunyizia tabasamu la huba.

“Mbona kama iko poteza raha. Iko problem?” alihoji Bi.Fahreen huku akimtazama Magosho usoni.

“Hapana mama niko sawa” alisema Magosho huku akiachia tabasamu la bandia.

“Najua Goso, mimi hapana penda ona veve kosa raha. Naleta hapa leo fundise gari” alisema Bi.Fahreen kwa sauti iliyokuwa imejaa upendo.

Maneno ya kufundishwa kuendesha gari yalizidi kumchanganya Magosho. Alikumbuka kuwa siku waliyofika eneo lile maneno yalikuwa ni yale yale na mwisho wake kukatokea balaa.

“Huyu mhindi wa watu leo atanifia. Sijui nikimbie?” Magosho aliwaza.

“Vipi mbona iko kaa kimya?” alihoji Bi.Fahreen.

“Niko sawa mama” Magosho alijibu huku akisubiria tukio ambalo lingefuata. Siku ile aliambiwa aende kukaa kwenye kiti kilichokuwa na usukani lakini asiteremke bali wapishane mule mule ndani ya gari, jambo ambalo mwisho wake likazua balaa.

“Basi kuje kae huku” alizungumza Bi.Fahreen. Magosho alitaka kushuka ili aende kukaa ule upande uliokuwa na usukani ambao alikuwa amekaa Bi.Fahreen.

“No. hapana veve suka, pitie hapa hapa” alizungumza Bi. Fahreen kama alivyozungumza siku hiyo ya balaa.

“Mnh!” Magosho akajikuta akiguna. Ni wazi balaa lililotokea siku chache za nyuma lilikuwa na dalili zote za kutokea tena kwa mara nyingine siku ile.



Pamoja na kwamba wezi walijitahidi kwa kadri ya uwezo wao na kufanikiwa kumrudisha nyuma Ashura kwa kumuibia, lakini binti yule hakukata tamaa hasa baada ya kupata faraja kutoka kwa kaka yake Magosho. Aliendelea na biashara ya kuuza vitumbua pamoja na kwamba biashara ya saluni ilisimama kutokana na kukosa mtaji wa kutosha. Enyi wezi popote mlipo Mungu awalaani!

Ashura akiwa amejikunyata barabarani akiuza vitumbua vyake, lilitokea gari ndogo aina ya STARLET na kusimama mbele yake. Alijiinua kwa haraka kwenda kumsikiliza akiamini kuwa alikuwa ni mteja wa vitumbua.

Mtu aliyekuwemo kwenye gari ile aliposhusha kioo Ashura akajikuta macho yakimtoka kwa mshangao. Alikuwa ni ZAWADI msichana ambaye alikuwa naye kwenye kijiwe chake cha kuuzia vitumbua siku za nyuma.

Zawadi alionekana kupendeza kuliko kawaida kiasi cha kufanya mtu aliyekuwa akimfahamu ashindwe kumgundua kwa urahisi. Zawadi yule aliyekuwa akiuza vitumbua na Ashura alikuwa ni tofauti kabisa na Zawadi huyu aliyekuja na gari siku hiyo. Walitazamana kwa sekunde kadhaa pasipo hata mmoja kati yao kuzungumza neno lolote.

“Zawadi!” alihamaki Ashura baada ya sekunde kadhaa.

“Ashura!” Zawadi naye akamuita rafiki yake.

“Ni wewe au naota?”

“Wala haupo usingizini!”

“Ni macho yangu au yana kasoro”

“Umzima wa afya tele”

“Nahisi utakuwa umeolewa na bosi Fulani hivi” Ashura alizungumza huku akimkodolea macho binti yule aliyewahi kuuza vitumbua pamoja naye.

“Kwanini unasema hivyo Ashura?”

“Wewe kapuku muuza vitumbua, hili gari ungelitoa wapi!”

“He! Shoga mjini mipango. Ukijipanga unatoka, usipojipanga unatokota” alisema Zawadi huku akitoa tabasamu. Aliingiza mkono wake kwenye pochi na kutoa noti tatu za shilingi elfu kumi kumi akamkabidhi Ashura.

“Chukua hii shoga, ngoja niwahi tutawasiliana” alisema Zawadi huku akiwasha gari yake.

“Haya shoga yangu, ila hongera sana” alisema Ashura huku akipokea ile hela aliyokuwa akipewa.

Zawadi aliondoa gari kwa mwendo wa taratibu na kumuwacha Ashura akiwa amesimama akimkodolea macho. Akawa kama vile alikuwa ndotoni kwa kile alichokuwa amekishuhudia. Akawa amezama kwenye lindi la mawazo. Binti yule amabaye hawakuachana sana umri ameweza kuwa na maendeleo ya haraka kiasi kile? Tena kamtaji kenyewe ka vitumbua kalikuwa hakajai popote.

Baada ya kujiuliza maswali mengi akapata jibu kwamba iliwezekana gari lile halikuwa lake. Lakini mtu bahili kama yule amewezaje kutuo pesa na kumuachia Ashura? Mh! Ashura hakupata jibu. Sauti ya mtu aliyekuwa akitaka kununua vitumbua ndiyo iliyomuibua kutoka kwenye lile dimbwi la mawazo.

*****

Magosho akajifanya hakusikia sauti ya Bi.Fahreen iliyokuwa ikimshauri wabadilishane siti za gari mle mle ndani pasipo kushuka. Aliteremka kwenye gari na kusimama nje ya mlango ambapo mama yule akajisogeza kwenye kiti alichokuwa amekaa Magosho kama abiria.

Magosho aliingia akakaa kwenye kiti cha dereva na punde zoezi la kufundishana kuendesha gari likaanza. Haikuwachukua shida kwasababu barabara ile haikuwa na magari mengi kiasi cha kuwaletea kero. Kwa kiasi fulani Magosho akarejewa na amani juu ya Bi.Fahreen. Akawa hana wasiwasi tena kwasababu mama yule alionekana kuwa mzima wa afya tele na hakuwa na dalili yoyote ile ya kuzimia.

Bi.Fahreen naye alionekana kuwa ni mwalimu bora kwa mwanafunzi wake. Lakini baada ya muda mfupi akaanza kufanya vituko. Ule mtandio mrefu aliokuwa amejifunga kiunoni aliutoa na kubakiwa na sketi fupi sana ambayo iliyaweka wazi mapaja yake kutokana na mpasuo wake mrefu uliokaribia kufika kiunoni. Magosho akajikuta akiguna ndani kwa ndani akihisi damu zikikimbizana mwilini mwake. Kwa kweli wacha zimkimbie tu, maana mwanamke yule wa kihindi alikuwa ameumbwa jamani! Sasa na ile nguo aliyokuwa ameivaa ndio kabisaaa.

Bi.Fahreen alimsogelea Magosho na kujifanya kuwa naye makini kwa kila hatua. Alizunguusha mkono wake wa kulia kweye mabega ya Magosho na kwenda kushika usukani. Kisha akamuinamia kiasi cha mashavu yao kugusana. Ndevu chache cha Magosho zilipomgusa Bi.Fahreen kwenye shavu lake akajikuta akipata raha fulani ambayo aliifahamu yeye mwenyewe.

Kwa upande wa Magosho nako mambo pia yalimuwia magumu. Bi.Fahreen aliupitisha mguu wake mmoja chini ya mguu wa Magosho na kwenda kukanyaga krachi ya gari. Akauchukua mkono mmoja wa Magosho na kuuweka juu ya paja lake ambalo lilikuwa wazi. Jamani mambo mengine ni kutiana majaribuni tu. Kama udereva wenyewe watu wangekuwa wanafundishana vile, sijui ingekuwaje huko barabarani.

Matendo aliyokuwa akiyafanya Bi.Fahreen yalimfanya Magosho kukumbuka vile vituko alivyokuwa akivifanya mama yule chumbani kwake siku moja alipomuita. Akakumbuka jinsi zigo la mama yule wa kihindi jinsi lilivyokuwa likitikisika na kutaka kudondoka hasa pale mama yule alipoingiza kichwa chake chini ya uvungu wa kitanda.

Magosho akajikuta mishipa yake ya damu kujaa kwa kasi na kukimbilia chini ya kitovu kiasi ya kupelekea kutengeneza uvimbe fulani ulioinua nguo yake kwa nguvu.

Bi Fahreen alipogungua kuwa damu za Magosho zilisababisha uvimbe kwenye mwili wake, alitoa tabasamu na kumtazama machoni kijana wa watu. Kwa kutumia mkono wake wa kuume aliushika ule uvimbe wa Magosho na kuanza kuuminya minya taratibu.

“Aaai! Mama!” Magosho alishituka na kuruka kwa nguvu kutokana na kitendo kile alichofanyiwa na Bi.Fahreen.

“Goso veve iko barikiwa sana” alisema Bi.Fahreen huku akiendelea kumshika shika Magosho kwenye ule uvimbe uliosababishwa na kujaa kwa damu.

Jamani Mambo mengine ni kutafutiana shida tu, pamoja na kwamba tunashauriwa sana kuwa makini na mazingira kama yale aliyokuwa amekumbana nayo Magosho, lakini vituko vile na mauzauza aliyokuwa akiletewa Magoshwa na mwanamke yule wa kihindi yalielekea kumshinda.

Pasipo kujielewa kijana Magosho alijikuta akijibu mashambulizi kwa kutumia ule mkono wake ambao Bi.Fahreen aliuweka kwenye paja. Alianza kupapasa lile paja jeupe la mama yule wa kihindi taratiibu huku akiumauma midomo yake ya chini kwa meno ya juu. Sijui ni kwanini kijana yule aliamua kufanya mambo kama yale, lakini sijui pengine ni kwasababu hakuwa anajielewa.

Kitendo kile alichokuwa amekifanya Magosho cha kuanza kujibu mashambulizi yaliyokuwa yameanzishwa na mama wa kihindi, kilizidi kumtia wazimu Bi.Fahreen kumfanya awe kama chizi freshi.

Mama yule alipeleka mdomo wake ambao ulikuwa karibu kabisa na mdomo wa Magosho kwa muda na kusababisha midomo ile miwili kukutana na kusabahiana. Baada ya Bi.Fahreen kuona dalili zote za kupata kile alichokuwa anakihitaji kwa muda mrefu, alijiinua na kusimama mbele ya Magosho.

Magosho akazunguusha mikono yake na kukamata mzigo mzito ambao ulikuwa ukimuelemea bosi wake na kumuwacha hoi kwa muda mrefu. Kwa viganja vya mikono yake akawa akilitomasatomasa zigo lile zito.

Masikini mwanamke wawatu wa kihindi akaonekana kuzidi kuchanganyikiwa na kuwa tena sio chizi bali ni mwendawazimu. Alipeleka mdomo wake kwenye sikio la Magosho na kutumbukiza ulimi wake kisha akaanza kuuzunguusha kama pangaboi.

Kwa kweli Magosho alikuwa amepatikana siku ile. Mama yule ambaye alikuwa amemzidi kiumri alikuwa akimuonesha vitu adimu kijana wa kizazi kipya.

Alichofanya Magosho ni kupeleka mikono yake juu na kukamata madafu ya mama yule na kuanza kuyachezea kwa kutumia vidole vyake vya mikono. Si haba sana, kwani hata Magosho naye hakuwa mbumbumbu mzungu wa reli kwani alijitahidi kwa kadri ya uwezo wake kudhihirisha uwenyeji katika majambozi.

“Aaaa! Goso…tar…tara…taratibu” alilalama mama yule wa kihindi huku ameukamata mkono wa Magosho akiuzuia usochomoke kifuani pake. Akili yake ilifanya kazi kwa haraka sana na kufyatua kiti kile cha gari ili kilale kiweze kuwapa nafasi ya kutosha. Mwanamke yule alikuwa amesahau kabisa kama alikuwa katika jitihada za kumnajisi mtoto wa mwanamke mwenzie.

“Oshsss!...mnh!..Goso…leo lazima veve jue endesa gali” alisema Bi.Fahreen pasipo kutambua alichokuwa anakizungumza. Ilikuwa kama vile mchezo wa kuigiza lakini ndiyo hali halisi iliyokuwemo mle ndani ya gari ya Mr. Nakeshwar.

* * *

Ashura alifanya kazi zake mapema sana siku hiyo. Alikuwa ameahidiwa na rafiki yake Zawadi kuwa angekwenda kumtembelea na kumchukua kumpeleka nyumbani kwake. Hamu kubwa ya Ashura ilikuwa ni kutaka kufahamu sabu iliyopelekea binti yule wa makamo yake kupata mafanikio ya haraka kiasi kile.

Akiwa chumbani kwake alisikia muungurumo wa gari kwa mbali. Akakurupuka na kutoka nje akitarajia kuiona ile gari ya Zawadi aina ya Stalet. Mambo yakawa tofauti kwani gari iliyokuwa ikitokea ilikuwa ni Rav 4 nyekundu. Ashura akasonya na kuingia ndani kwa kisirani.

Gari ile ilifika na kufunga breki nje ya nyumba ile aliyokuwa amepanga Ashura. Ilipiga honi mara kadhaa lakini Ashura hakutoka ingawa alikuwa akiisikia. Baada ya dakika kadhaa akasikia mlango wa chumbani kwake ukigongwa. Alijiinua kwa hasira akiamini wapangaji wenzake ndio walikuwa wakimgongea.

“He Zawadi !” Ashura akajikuta akihamaki baada ya kufungua malngo.

Kumbe aliyekuwa akigonga mlango alikuwa ni rafiki yake ambaye alikuwa akimsubiri kwa muda mrefu pale nje.

“Jamani shoga, ndiyo nini mwenzio kupiga honi halafu ukanikaushia?” alihoji Zawadi huku akiingia chumbani kwa Ashura.

“Kwani wewe ndio uliyekuja na hiyo Rav4 nyekundu?” alihoji Ashura kwa hamasa kubwa iliyokuwa imechanganyikana na mshangao.

“He! kumbe umeniona. Sasa mbona umenifanyia hivyo shoga yangu?” alihoji Zawadi huku akijiweka kwenye kitanda kidogo cha Ashura.

“Shoga nilisikia muungurumo wa gari nikatoka nje, sasa nilitegemea kuliona lile gari ulilokuja nalo siku ile, nilipoliona hilo nikanuna na kuamua kuingia ndani nikiamini kuwa sio wewe.” Ashura alijitetea kwa maelezo mafupi.

“Haya basi yameisha shoga yangu. Enhee niambie” alizungumza Zawadi huku amkimkodolea macho Ashura.

“Umependeza Shoga yangu utafikiri mtoto wa kigogo Fulani hivi” Ashura alizungumza kwa kumsifia Zawadi huku akimtazama kwa tabasamu zito lililokuwa limejaa matumaini.

“Haya Shost ahsante, lakini ni kawaida yangu kupendeza” alizungumza Zawadi kwa majivuno.

“Hongera mwaego”

“Nashukuru. Unajipya gani Shost yangu?”

“Nilitoe wapi? labda nikuchemshie chai ya rangi na vitumbua unywe” alisema Ashura.

“Akaa! Chai na vitumbua vyako kunywa mwenyewe shoga”

“Najua umeshazoea mchemsho wa kuku” Ashura alizungumza kwa utani.

“He! Umejuaje shost. Mwenzako chai ya asubuhi wala siiwezi”

“Mnh! Shoga huo mchemsho utakunywa nyumbani kwako. Ukija kwangu mwendo wa chai ya rangi na kiporo cha wali” alisema Ashura huku akicheka. Alichokuwa anakizungumza alikuwa akimaanisha, hali ya ya Maisha yake haikuruhusu kula chakula alichokuwa akikitaka Zawadi. Na kama angethubutu kuweka bajeti ya kula huo mchemsho kila siku basi kamtaji kake kote kangeyeyuka kama barafu lililokuwepo kwenye joto kali juu ya jabari.

“Usijali sana shoga. Kwanza hapa nilipo kitumbo kipo ndii!”

“Haya Hebu tuwachane na hayo Shoga” alisema Ashura huku akionekana kama vile kulikuwa na kitu alichokuwa anataka kukizungumza.

“Enhe lete jipya”

“Shoga naona jinsi mambo yako jinsi yalivyo kuwa super”

“Kwanini Shost?”

“Unabadilisha magari kama nguo! Juzi ulikuja na Stalet, leo umekuja na Rav 4, sijui kesho utakuja na nini” alisema Ashura kwa masihara.

“Ah! Ni vijimambo tu hivi Shost” alisema Zawadi huku akiangalia angalia mle chumbani mwa Ashura kama vile kulikuwa na kitu alichokuwa anakitafuta.

*****

Magosho na Bi.Fahreen walikuwa wakiendelea kupagawishana mle ndani ya gari ya Mr. Nakeshiwar. Walijikuta wamehamia viti vya nyuma ili kuweza kuwa huru zaidi kufanya mambo yao. Magosho akiwa juu ya Bi.Fahreen aliweza kuruhusu viganja vya mikono yake kutalii kila kona hatari katika mwili wa mwanamke yule wa kihindi.

Mama yule alijikuta akipagawa kila mahali ambapo vidole vya Magosho vili pita. Kuna wakati alikuwa akitamani visihame sehemu nyingine lakini vilipohama na kugusa sehemu nyingine alijikuta akipata raha zaidi na kutamani viendelee kuwepo pale pale.

“Goso…mimi…iko taka oa veve” Bi.Fahreena alikuwa akizungumza pasipo kujielewa. Inawezekana ni kutokana na mambo aliyokuwa akioneshwa na Kijana.



Magosho alikuwa kama vile mtu aliyepandwa na mapepo, alikuwa hasikii wala haoni. Alikuwa amekwisha sahau mateso aliyoyapata siku aliponusurika kufumaniwa na bosi wake akiwa na huyo huyo mwanamke chumbani. Waswahili wanasema sikio la kufa halisikii dawa, nadhani hata kijana Mangosho ndio hao hao.

Bi.Fahreen alipeleka mkono wake na kukamata shingo ya mjomba bubu na kuanza kumsugua taratiibu kwa uwangalifu na ufundi mkubwa. Magosho akaonekana akitulia na kusikilizia kama vile alikuwa anamwagiwa maji ya baridi mwilini.

“Aaaaiiyaaa!….omnh…ngoja!….ngoja kwanza Fahre” Magosho akajikuta akipiga kelele huku akiushika mkono wa Bi.Fahreen kujaribu kuuondoa. Hata hivyo mama yule akaonekana kuto kujali kilio kile kwani aliendelea na zoezi lake.

Magosho akashusha mkono wake hadi kwenye tumbo la mama yule ambalo kwa wakati ule halikuwa na kizuizi chochote. Akatumbukiza kidole chake cha kati kwenye kitovu cha mama yule ambacho kilikuwa kimetumbukia ndani na kuanza kukizunguusha kimduara.

“No!...Goso….No!...Hiyo…aaah….usitoe amnmh!…ooioo..,yes..uuh!” Bi.Fahreen alijikuta akikosa nguvu na kuachia shingo ya mjomba bubu.

Magosho aliteremsha mikono yake chini ya kitovu cha Bi.Fahreen na kuruhusu vidole vya mikono yake kufanya kazi ambayo yeye alitaka vifanye. Zoezi lile ndilo lililoonekana kulimaliza kabisa jimama lawatu la kihindi na kusikika likilalama.

“Oosss….Aaasss…Mnh! tamu Darling…” sauti ya Bi.Fahreen ilitoka kwa shida.

Magosho alizidi kumpa vitu mama yule aliyeonekana kushikika ipasavyo. Hakupenda kuichezea nafasi ile ambayo alikuwa akiitamani kwa muda mrefu na hakuwahi kuwa na ndoto ya kumpata mama yule wa kihindi.

Pepo la mahaba lilikuwa limnempanda vilivyo Magosho kiasi cha kutojitambua kwa kila alichokuwa anakifanya wakati ule. Vidole vya mikono yake viliendelea kufanya kazi kwenye mwili wa mke wa bosi wake na kumfanya mama wa watu kuendelea kulalamika na kuomba msaada.

“Goso… iko…iko tosa sasa….tibia mimi bhanaa” masikini ya mungu mwanamke yule aliendelea kutoa sauti za vilio vya kuomba msaada kutoka kwa kijana wake wa kazi.

“Sawa baby” Magosho akaunguruma.

“Goso…au veve taka mimi kufe?”

“Usiwe na haraka mpenzi ntakutib…Aaaah!” Magosho alijikuta akishindwa kumalizia sentensi yake kwasababu Bi.Fahreen alipeleka mkono wake na kumvuta Mjomba bubu ghafla kulazimisha msaada.

Magosho alipojitambua aliendelea na shughuli ya kumpagawisha mama yule kwa michezo ya kibantu. Loo! Kumbe kitendo cha kumvuta mjomba bubu kilizidi kumpa midadi Magosho ya kufanya mashambulizi. Bi.Fahreen akajikuta akiwa hoi bin taaban, hajitambui wala hajielewi.

“Goso... tibia bhana…roho iko kimbia sasa”

“Nakupa mama...nakupa…amnmn…nakupa….oshssss! Magosho naye alikuwa akijilalamisha kivyake huku akiendelea kuchelewa kutoa msaada kwa mwanamke wa watu wa kihindi.

“Sasa…mbona iko chelewa veve?” masikini mwanamke yule aliendelea kulalamika. Nafikiri alikuwa katika wakati mgumu zaidi ya hata tunavyofikiria mimi na wewe msomaji wangu.

“Usihofu Fahreen, leo mimi ni wako na wewe ni wangu” Magosho naye akaungumruma. Nafikiri siku hiyo alikuwa amedhamiria kufanya mauaji ya kukusudia.

“Acha mineno mingi bhanaaa… nguvu…iko…iko…kwisaaa” alizungumza Fahreen kwataabu na kigugumizi kizito kilichosababishwa na shughuli ya Kijana wa kibantu.

Magosho akanyamaza kimya kama vile hakumsikia mke wa bosi wake alivyokuwa akilalamika kwa shida. Yeye alikuwa bize na kucheza na mwili ule adimu wa mwanamke wa kihindi. Bila ya huruma alizidi kutalii kwenye kona ambazo zilikuwa hatari zaidi na kusababisha Bi.Fahreen kuhisi karaha badala ya raha.

*****

Macho ya Zawadi yaliendelea kutarai mle chumbani mwa Ashura huku uso wake ukionekana kupendeza kwa tabasamu. Ashura akamsemesha.

“Usishangae Shoga, haya ndiyo Maisha yangu”

“Dah, hiki chumba kinanikumbusha mbali sana” alizungumza Zawadi kwa nyodo na majivuno ya hali ya juu.

“Wenyewe tumeshazoea kuishi na buibui pamoja na mijusi ndani”

“Haya sio Maisha Ashura shoga yangu jitahidi uyatoke” alisema Zawadi kwa sauti ya kujiamini iliyokuwa imejaa kejeli na majivuno.

“Nitayatoka tu, kikubwa ni kumuomba Mungu Shoga” Ashura akajibu kwa unyonge kwasababu aliamini wazi jambo la kuyatoka maisha yale halikuwa linawezekana kirahisi vile.

“Pamoja na kumuomba Mungu, lakini unatakiwa ujitume” Zawadi alizungumza kwa msisitizo huku akitafuna jojo.

“Shoga yangu ninajituma sana lakini maisha bado yamebana” Ashura alielza.

“Tatizo lako shoga Maisha unayanunia na ndiyomaana na yenyewe yananuna” alisema Zawadi.

“Mnh! Shoga hujaacha tu maneno yako?”

“Habari ndiyo hiyo Shoga. Maisha ukiyachekea na yenyewe yatakuchekea” alizungumza Zawadi huku akijiinua kutoka pale kwenye kitanda na kusimama mikono ikiwa kiunoni.

“Vipi mbona hivyo?”

“Tuondoke, au bado hujajiandaa?” alisema Zawadi.

“Ah! Mie nipo tayari Shoga au sija pendeza?” Ashura alizungumza huku akijitazama mara mbilimbili kutaka kusikia neno kutoka kwa shoga yake yule.

“Umetokelezea Shostito” alisema Zawadi na kutoka nje.

Ashura alipofika nje alimkuta Rafiki yake amekwisha ingia kwenye gari. Na yeye akajipakia mbele na safari ikaanza.

“Lakini Zawadi mbona hufunguki?” alizungumza Ashura gari ilipokuwa ikiendelea na safari.

“Nifunguke Manini tena shoga” alihoji Zawadi huku akikanyaga mafuta na kuzunguusha usukani kwa mbwembwe za kisistaduu.

“Umepata buzi gani linalokuhonga magari haya?” Ashura alihoji kwa umakini mkubwa.

“Wala hakuna mwanaume anayenihonga shoga”

“Sasa pesa umetoa wapi?”

“Ni kazi ya mikono yangu mama”

“Kazi gani unafanya?”

“Mambo mazuri hayataki haraka”

“Haya bwana, mdomo koma”

“Tena ukome ukomae” alizungumza Zawadi na kufanya wote wawili kuangua kicheko kisichokuwa na maana yoyote.

Macho ya Ashura yalikuwa hayatulii mle ndani ya gari. Alikuwa akilithaminisha na na kumwaga masifa kwa rafiki yake yule wa siku nyingi. Mziki mkubwa ulikuwa ukiwaburudisha walipokuwa njiani. Ashura akajiona ni mtu mwenye ngekewa ama kismati kwa kupata bahati ya kupanda gari kama lile. Siku zote alikuwa akiyaona tu barabarani yakimpita kwa mbwembwe.

Gari ile ilikwenda kufunga breki nje ya geti la jumba moja kubwa lililoonekana kuwa la thamani sana. Geti lilipofunguliwa na mlinzi Zawadi akaliingiza na kwenda kulipaki pembeni ya magari mengine yaliyoonekana kuwa ya kisasa kuliko yale aliyokuwa akiyafahamu Ashura. Zawadi akamtaka Ashura wateremke kwani walikuwa wamekwisha fika safari yao.

“Zawadi” Ashura aliita kwa sauti ndogo.

“Niambie Shosti”

“Unaishi hotelini?” Ashura alihoji huku akishangaa shangaa yale mazingira. Zawadi alicheka kidogo kabla ya kuzungumza neno lolote kujibu swali lile la rafiki yake..

“Hii sio Hotel Shost”


ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

BLOG