Search This Blog

Wednesday, January 25, 2023

NYOO NIPE MUMEO - 5

  

Chombezo : Nyoo Nipe Mumeo

Sehemu Ya Tano (5)


Nikakumbuka yale maneno yanayosemwaga kuwa ukiona mpenzi wako anakwambia kila mtu anayemtongoza, jua kuwa ni kwa sababu hamtaki, lakini akimtaka hatathubutu kukwambia.

Hivyo ilikuwa wazi kuwa Fatuma alikuwa akinipindua ndiyo maana mume wangu hajaniambia, hasira zikanipanda mara dufu, nikachukua maji mengi na kunywa mfululizo, hii inasaidia kupunguza hasira.

Muda huohuo nikamuona Gululi akitoka bafuni nikajifuta haraka michirizi ya machozi, akapita na kuingia ndani kama kawaida yake akiachia tabasamu pana.

Baadaye alitoka na kanga na kuja kukaa pale kwenye kiti, akaniuliza kama nimeivaa ile dawa, nikamwitikia kwa kichwa tu. Lakini nikakumbuka kuwa bado hakunimalizia kuhusu ile elimu ya shanga kuna rangi bado alikuwa hajanimalizia. Maana nilizozikumbuka ilikuwa nyeupe na nyekundu tu na tulikuwa tukitaka kuzungumzia shanga ya rangi nyeusi.

Basi akaenda kubandika sufuria la maji jikoni na kuwasha jiko la gesi nililowanunulia, akanipa ungo nichambue mchele wakati yeye anaandaa samaki kibua.

“shanga za rangi nyeusi huvaliwa pale mwanamke anapokuwa yupo tayari kumpa mwanaume wake raha na utamu lakini tatizo inakuwa bado hujanyoa bustani kutokana na dharula yake, kwa hiyo kwa mwanaume mjanja anayeelewa hivyo, unakuta anaweza kumsapraiz mwenzake kwa kukunyoa, lakini kama amepandwa na hamu anaweza kuingia hivyohivyo korokoroni.” Alisema Gululi jambo ambalo lilinifanya niwe na mtazamo upya kuhusu shanga. Nikatamani niwe nazo na mimi nimvalie Mr X.

“lakini mbona kuna wengine wanavaa nyingi tena zina rangirangi tofauti hizo zinamaanisha nini?”niliuliza nikikumbuka picha moja hivi niliionaga kwenye mtandao ya mwanamke akiwa na shanga kibao kiunoni.

“hizo za rangirangi ni kwa ajili ya urembo tu kuongeza mautamu kitandani kama nilivyokwambia mwanzo. hazina maana yoyote ile. “unajua kiuno cha mwanamke kimeumbwa na hisia za kimahaba na ndio maana ukikitomasa au ukikipapasa lazima mwanamke ajisikie raha.


NYOO NIPE MUMEO 62

“Ukiwa na zile shanga nyingi mwanaume akikuchezea kiunoni kwa mikono yake utajisikia kutekenywa fulani hivi kama anakuwasha moto na wewe uchochee kumnyongea viuno.” Alisema Gululi.

“Mh sasa nimeelewa, lakini mbona kuna wanawake wengine wanazivaa hata barabarani! utaona kwenye viuno vyao kuna shanga tele, kwa nini wasivae tu chumbani?”niliuliza.

“tunasisitizwa sana kwenye kuvaa tuhakikishe nguo zinazificha shanga kwa sababu zinatakiwa kuonekana na mpenzi wako tu, siyo kwingineko.

“unajua kuna wengine wamevamia tu nao wanataka kuvaa shanga ndiyo unakuta mtu kavaa shanga nyeupe lakini ndani ana minywele kama msitu, mwingine anavaa nyekundu wakati hayupo kwenye siku zake haya yote ni kutokana hawajapitia unyago. Mimi angalau kidogo mama alikuwa akiniambia,” alisema Gululi.

Wakati tumeshamaliza mapishi kigiza kikianza kuingia mara nikaona simu ya Catherine inaingia. Nikashangaa nikapokea.

“Shoga mzima? Upo wapi? nasikia siku hizi unaiva na Hadija tangu lini?”

“kwani vibaya? Angalau yeye si mnafiki kama nyinyi wa kunificha yanayotendeka mbele ya machoyenu,” nilimshushua.

“najua Mary, lakini wewe unafikiria tungeanzaje kukwambia, halafu isitoshe mama yako mwenyewe alitukataza tusikwambie!” alijitetea Cathe.

“lakini hata hivyo wewe ni shoga yangu, siyo wa kunificha, unajua imeniuma sana!”

“najua shoga imekuuma lakini mama hali yake ipoje.. maana! aisee wanaume sijui wapoje? Simuongelei vibaya baba yako lakini naye atuliege maana kazidi!”

“baba angu? Kwani kafanya nini?” niliuliza kwa mshangao.

“He! kwani Mary vipi mbona sikuelewi? Kwani hapa tunamuongelea nani?”

“ si mume wangu au!”

“mume wako kafanya nini!”

“hebu nieleze vizuri, nyinyi si mmenificha kuhusu mume wangu kutembea na Fatuma au?”

“mumeo naye katembea na …. mbona hiyo mpya siijui! Na mumeo anatembea na Fatuma? Lini shoga! Mbona mkosi huu,” alisema Cathe akawa amenichanganya.


NYOO NIPE MUMEO 63

“Au mimi nitakuwa ndiyo nimejichanganya? Kwani siku ile wakati nimelewa ilikuwaje?” niliuliza ili nipate vizuri.

“Ha! Siku ile baba ako alikuwa amebwia hadi staha zake zikamuisha, akaanza kushikanashikana na Fatuma mbele ya mama yako mwanzoni tulidhania utani. “Wakati huo wewe ulikuwa umelewa mno ikabidi mumeo akubebe na kukurudisha nyumbani. Halafu akarudi kuendelea kufurahi na sisi, lakini tulishangaa kutomuona baba yako wala Fatuma, ndiyo mama ako akarudi nyumbani akihisi pengine mumewe ametangulia.

“Huwezi amini tulimuona mama yako anakuja kwa hasira huku akilia, tulipofuatilia ndiyo tukamkuta baba yako uchi wa mnyama na Fatuma kwenye ile midizi ya pale nyumbani kwenu wakifanya uchafu wao.

“Mbaya zaidi, eti baba yako baada ya kutuona ndiyo kwanza akawa anampiga mama ako, wakati kosa ni lake. Uzuri shemeji yetu Mmarekani ndiyo akaingilia akambana baba ako na kumrudisha nyumbani, yaani ilikuwa mtiti wa maana. Fatuma alikimbia lakini asivyo na aibu yule msichana nasikia anatembea mtaani shingo juu kama hakuna kilichotokea na mumeo hasikii aambiwi!” alisema Catherine.

Nikashangaa, kwa sababu mimi siku zote nilikuwa nahisi ni mume wangu ndiye aliyekuwa amefanya uchafu ule na Fatuma kule vichakani! masikini kumbe nilikuwa nikimuonea tu.

“enhee sasa niambie na huyo mumeo alitembea naye saa ngapi?” aliuliza Cathe, ikabidi nimwambie kinagaubaga nilivyokuwa nikijua mimi. “He! Shoga kweli ulikuwa unajishtukia, yaani Fatuma atembee na mumeo! Haa ndiyo maana umekimbia nyumbani? Hee wa Mary mumeo alivyo mstaarabu vile,” alisema Cathe. Huwezi amini nikaona aibu mno kwa kukurupuka kumhisi mume wangu vibaya kwa uchafu wa baba.

Nikavuta picha ndiyo nikakumbuka siku zile niliposikia mama akigombana na baba asubuhi, na siku nyingine baba alipokuwa akikwaruzana na mume wangu. Nikakumbuka siku ile mama aliponihusia kuhusu wanaume hadi akawa anatoa machozi.

Jamani kumbe mama yangu ndiye aliyekuwa akiumia muda wote.


NYOO NIPE MUMEO 64

Nilinyanyua simu na kumpigia, akapokea huku nikisikia kabisa sauti yake ikilazimisha furaha baada ya kunisikia.

“mama, kwa nini ulinificha!.. kumbe baba yupo hivyo” niliuliza huku machozi yakinitoka kiasi kwamba hadi Gululi alinishangaa.

Kwa kuwa ilikuwa ni usiku kidogo nilishindwa kurudi nyumbani japo kuwa nilitamani, na isingekuwa vizuri kuondoka bila Bibi. Gululi kuwepo nyumbani pia.

Kwa jinsi nilivyokuwa na huzuni, nilishindwa hata kumjibu Gululi ambaye alikuja karibu yangu na kunibembeleza.

Lakini bado nilikuwa najiuliza inawezekanaje sasa kama mume wangu hahusiki? aliwezaje kufika pale dukani na kumnunulia Fatuma kitenge?

Nikajua siwezi kupata jibu la swali langu kama sitampigia mume wangu, nikamuendea hewani, kama kawaida yake hakuwa akichelewa kupokea hususani kama mimi mkewe ndiye niliyepiga simu, yaani hata kama akiwa anaongea na nani lazima akate tu kwanza na kunisikiliza mimi.

“hallow wife,” alinipokelea kwa bashasha.

“kuna nini kati yako wewe, baba na Fatuma,” niliuliza.

“ooh nadhani nimeshajua sababu ya wewe kuondoka nyumbani. Lakini kwanini uliamua kuondoka wakati ulitakiwa kubaki nyumbani kumbembeleza mama kwa yote yaliyotokea?” alianza kunihubiria sasa; nikatamani kumwambia sikufahamu hayo kabla lakini nikaamua kuweka swali langu liwe specific zaidi maaana niliona kama hanielewi.

“acha hayo, ninachotaka kujua kwanini wewe unaendelea kukutana na Fatuma wakati unafahamu ndiye anayeharibu ndoa ya baba?”

“Najua utakuwa bado hauelewi mengi kuhusu baba yako na sikuwa nimetaka kukwambia kwa sababu ni mambo mazito ambayo sikudhania kama baba yako anayafanya. Kama utataka tuongee, rudi kesho,” alisema mume wangu akionekana moyo wake mzito kweli.

Nikawa nawaza kuhusu hayo maneno aliyosema kuwa kuna mengi kuhusu baba ambayo ni mazito. Nikakumbuka maneno ya Hadija kuwa baba yangu alishawahi kumtongoza na alikuwa akitumia hela zote tulizokuwa tukimtumia kwa starehe na visichana vidogo kama Fatuma.


NYOO NIPE MUMEO 65

Nilijisikia vibaya sana na kupanga mapema kesho nitaenda nyumbani lakini kama kawaida darasa litaendelea maana hata kama sasa nimeanza kupata ukweli kuwa Fatuma hatembei na mume wangu, vipi kama atatokea mtu mwingine kama Fatuma au zaidi akaja kunipindua siku za mbeleni, lazima niwe imara.

Basi wakati nikiwa na mawazo hayo, bibi Gululi aliingia akionekana na furaha mno, akaja kukaa pale nilipokaa mimi na haraka akagundua huzuni yangu.

“bibi kuna tatizo nyumbani kesho itabidi niende kwanza nikalimalize,” nilimwambia, hakutosheka, akanidadisi.

“kuhusu mumeo?”

Nikajibu kwa kuitikia kwa kichwa. Kwa jinsi alivyoniangalia nikaona ngoja tu nimueleze maana sina mtu mwingine wa kunisaidia nikamueleza kila kitu nilichokisikia kutoka kwa rafiki yangu.

“He kwa hiyo kumbe Fatuma anatembea na baba yako! He mtoto amejaa laana yule! Lakini ni kheri kuliko ndoa yako changa. Enhe sasa?” Alisema bibi Gululi huku akionesha kunionea huruma.

“bibi bora hayo, leo ndiyo mume wangu ananiambia kuwa Hadija ameanza kujitongozesha kwake na amekuwa akimwambia kila kitu tunachokifanya huku!” niliamua kuvunja ukweli.

“Mungu wangu! Nilijua tu Hadija ana macho mawilimawili yule mtoto anatoka Fatuma anaingia huyu, lakini mwanangu usihofu Hadija hajui kitu hawezi kukuzidi kwa chochote,”

“mh mama inawezekana! Lakini Hadija mshirikina sana, hapa ndiyo napata picha sasa, maana tulipokuwa chumbani alikuwa akijihangaisha kuongea kingereza na mtu kwenye simu, tena baadaye akaniomba nimuelekeze kuangalia jina la mtu tigopesa na kuna namba alikuwa akiiangalia jina lake, nahisi anapeleka kwa mganga kuroga na kama siyo la mumeo sijui?” alisema Gululi.

“nini? namba yenyewe ni ipi? Jina gani lilikuja?” niliuliza harakaharaka kwa hofu.

“Nadhani inaishia 99, sijaikariri sana,” alisema Gululi wakati huo namba ya mume wangu ilikuwa inaishia hivyohivyo 99. Ina maana kweli anaenda kunirogea mume wangu ili ampende! Jamani hawa waswahili nimewakosea nini mimi.

Itaendelea..


NYOO NIPE MUMEO 66

“Hebu wewe Gululi umsitie presha mwenzako, labda namba sio hizo zimefanana tu mwishoni.” Alisema Bi Gululi.

“mh na kingereza alichokuwa akiongea humu ndani? mama wewe mwenyewe unajua ukienda kwa mganga cha kwanza lazima atakwambia umtajie majina kamili ya mtu unayemtaka.

“Tena nasikia Hadija siyo mtu yule, hata huyo mumewe si alimpata kwa madawa, madawa yameisha ameachwa,” alisema Gululi, wakawa wananichanganya maana mwenzao hayo masuala ya waganga nilikuwa siyaamini na wala siyajui.

Niliamua kuwa mkimya na asubuhi nikaamka mapema nikafanya usafi, nikaoga na kuvaa nguo zangu, lakini lile begi langu nililiacha kwa kuwa nilipanga lazima nirudi kumalizia mafunzo yangu.

Nikawaaga vizuri tu na kutaraji kurudi baada ya siku mbili hivi.

Niliingia nyumbani nikawakuta wote wapo pale sebuleni kasoro baba tu, nadhani alikuwa kwenye umalaya wake huko mtaani. Nilimfuata mama na kumkumbatia huku machozi yakinitoka. Kuona hivyo wote waliondoka pale sebuleni.

“mama kwa nini haukuniambia!” nilisema kwa uchungu kwa kuwa najua maumivu ya kusalitiwa, of coz kwa kuwa nilidhania mimi.

“mwanangu tuache hayo, ni hulka tu za baba ako siku hizi, ila naomba tu mwache aendelee na mambo yake, wewe na mumeo nataka mfanikishe yote mlioyoyajia,” alisema mama sasa ndiyo nikaona vizuri uso wake ulivyojaa huzuni.

Tena akikonda mno kwa mawazo, ngozi yake nyororo niliyorithi kutoka kwake ilikuwa imesinyaa na kupoteza mvuto kabisa.

“yameanza lini haya!” niliuliza nikijaribu kuunganisha maneno ya Hadija kuwa kipindi chote tunapotuma hela huku nyuma baba alikuwa akizitumia kufanya uchafu wake.

Lakini hata nilipojitahidi kuongea naye mama alikuwa amejizatiti kweli kutoongea chochote, ni wale wanawake waliofunzwa kizamani, kuwa wavumilivu hata waume wao wawafanyie kitu gani.


NYOO NIPE MUMEO 67

Aisee moyo huo mimi sina, nilikuwa tofauti aisee, kwa muda mchache tu nadhani mmeona nilichoweza kufanya.

Sasa kwa kuwa mama haongei, mtu mwingine wa kumalizana naye alikuwa ni mume wangu na nilikuwa na maswali mengi mno kwake.

Nilimfuata huko nje nikamuona anacheza na Kendrick, mtoto wangu aliponiona tu akatabasamu na kuongea maneno yake yasiyoeleweka, nikamnyanyua na kumbusu kwa nguvu nikilipiza siku zote ambazo nilikuwa nimemmiss mno.

Nikiwa nimembeba mwanangu, mume wangu naye akawa anakuja eti anikumbatie, nikajitoa kwanza kwa sababu nilitaka anieleze, tena anieleze uzuri, nimuelewe ndipo tuive sahani moja.

“haya kwanza niambie yote uliyosema utanieleza!” nilimwangalia kwa ukali akaanza kunielezea taratibu.

“kiukweli, siku ya pili tu baada ya kufika hapa kwenu, nilianza kuona tabia ya baba yako kuwa siyo nzuri. Kuna kipindi tulipotoka kutembea alikuwa akinitambulisha mademu zake na tena akinitaka niwalipie bili au kuwanunulia vitu mbalimbali. “Nilikuwa sipendi kukwambia lakini I’m so ashamed,” alisema mume wangu kwa uchungu kidogo nikalegeza ukali nikamsogelea na kumshika bega.

“nilikuja kugundua kuwa anatembea na rafiki yako yule mwembamba, na hadi sasa ninavyokwambia, huyo msichana ana mimba changa na baba yako ndiyo anahudumia kila kitu,”

“Nini Fatuma anamimba ya baba?” nilihamaki lakini Jermaine akanizuia nisiongee kwa sauti kwa kuwa mama hakuwa akijua hayo. “siku akiwa amebanwa ananituma mimi hadi kumnunulia mahitaji ya huyo mtu wake, tena kwa hela yangu mimi,” aliendelea mume wangu.

“kwa nini haukuniambia?”

“ningeanzaje?” “na huyo Hadija ilikuwaje!” nilibadilisha swali.


NYOO NIPE MUMEO 68

“Alikuja hapa nyumbani wakati wote tuna hofu juu ya sehemu uliyoenda, ndiyo akaniambia kuwa upo nyumbani kwake ndo maana nilimpa namba yangu ya simu ili tuwe tunawasiliana. Lakini amekuwa akiniambia mengi kuhusu wewe kuwa umetoroka na mwanaume, unanisaliti lakini nia yake nilikuja kuijua baada ya kuanza kuonesha kunitaka!”

Kwa maneno hayo nilijikuta nikishindwa kufanya chochote, zaidi furaha kubwa ikanirudia moyoni kuwa kumbe mume wangu hakuwa akitembea na Fatuma, nikasimama na kutanua mikono nikiruhusu aje anikumbatie, naye akasimama na kunikumbatia kwa nguvu.

Palepale nikampa nyama ya ulimi, likawa siyo kumbatio tena badala yake ni mpapaso wa nguvu, kila mmoja akionekana kuwa na hamu na mwenzake.

Kiukweli hatukuweza kufanya chochote pale nyumbani kwa kuwa mama alikuwepo na siyo vizuri, nilifanya ujanja wa kumkabidhi Kendrick kwa dada na kutoroka na Mr X wangu tukaenda kwenye Hoteli moja hivi pale Kimara.

Tuliingia ndani yaani ilikuwa kama vile ndiyo tumeanza mapenzi upya. Sasa nikapania kumuonesha Mr X kidogo tu nilichojifunza kwa kungwi.

Itaendelea..


NJOO NIPE MUMEO 69

Nilipoingia tu kwanza nilitaka kumshangaza, nikaingia bafuni na kuoga peke yangu, halafu nikavaa shanga nyeupe nikianza kwa kukopi njia zote za Fatuma kama alivyonisimulia Steve siku ile.

Nikavaa taulo na kutoka nikamtaka na yeye aingie bafuni kwa ajili ya kujisafisha maana nilikuwa nimempania mno. Hakuchukua muda mrefu si unajua wanaume wanavyoogaga chapchap tena wakiahidiwa mchezo.

Basi alipofika tu pale kitandani. Nikamtaka atulie kwanza, wakati huo mimi nikaketi kwenye kimeza kidogo kilichopo pembeni ya kitanda nikaanza kujipapasa mwili wangu taratibu kama vile najipaka losheni.

Nikaanza kujivua taulo polepole huku kifua changu kikiwa wazi sasa nikaanza kuyashika manido yangu na kuyanyanyua huku nikijifanya sina habari. Hayo yote nilikuwa nimeiga na kuboresha ujanja wa Fatuma ambapo humfanya mwanaume amtazame wakati yeye anafanya sarakasi uchi.

Kwa kuwa mimi sarakasi siwezi ngoja nimtege Mr X kwa mtindo huo, nikamuona alivyokuwa akiniangalia kwa kunitamani lakini tamaa hiyo ndiyo niliyokuwa nikiitaka kwa sababu mwanaume akikupania ndiyo mapenzi yanakuwa matamu na yeye ataridhika mapema kuliko kufanya mapenzi tu kawaida.

Niliona alivyoanza kushangaa baada ya mimi kuvua taulo lote na yeye kuona zile shanga kiunoni. Nikaunyanyua mguu wangu mmoja na kumfanya aone utamu wote ukiwa umejichanua mbele yake. Lakini bado nikaanza kujichezea mwenyewe nikizungusha kidole changu taratibu karibu na nekta ya ua rangu la waridi, nikajigusa kiyoni changu na kuanza kukisugua taratibu kama vile Dj anavyosugua CD.

Nikamtazama Mr X kwa jicho la kuibia nikamuona akisogea taratibu, nadhani hakuwa akitaka nijue kama ameshindwa kuvumilia kusogea.

Basi kile kidole changu nikaanza kukiongezea manjonjo ya kukikatikia, halafu nikajifanya naugulia kwa utamu wake huku nimefumba kabisa na macho.


NYOO NIPE MUMEO 70

Ghafla nilihisi mkono mzito ukianza kunipapasa mapajani, nilijichekea kimoyomoyo kuona mbinu yangu imefanya kazi, yaani Mr X alikuwa ameinuka mwenyewe kutoka kitandani na kunifuata hadi nilipo, tena akiwa ameshasimamisha mtalimbo hatari.

Hapa niwape siri wanawake, yaani kwa mtindo nilioufanya mimi hata kama mwanaume yupo Kimara na wewe upo Mbagala, ukimuonesha hivyo lazima apande gari kukufuata unakuwa umemchanganya kweli kiasi kwamba kichwa chake cha juu kinagoma kufanya kazi na kichwa chake cha chini sasa ndiyo kinampelekapeleka.

Basi kwa nikamuona Mr X akaanza kunibusu mapajani huku taratibu mdomo wake akiupeleka Uvinza.Jamani hapo hata kama mwanamke ni fundi vipi, kama mwanaume ukifika hapo, huyo mwanamke hana chake tena. Tena kwa ile hewa yake ya motomoto alivyokuwa akinipumulia kule chini nilianza kujisikia kusisimka kwa ajabu.

Nikawa natamani aanze kuonja chumvi, maana alikuwa akinibusubusu tu kuzunguka kipapatio changu kama dakika nzima. Huwezi amini juisi ya mahaba ilikuwa imeshaanza kunimwagika.

Hapana sikutaka nilainike kiasi hicho lakini utamu wa mchezo wake ukanifanya nishindwe kujizuia nikamkamata kichwa chake kwa nguvu na kumshusha chini kwenye kiyoni changu.

“nichezee hapooo,, aaahhhhh!” nilitoa maelekezo kwa sauti ambayo hata sikujua kama ilinitoka akaanza kuninyonya kama anavyonyonyaga, nikajipinda kufuata utamu ulipo basi Mr X alivyokuwa mjinga akawa ananinyonya huku anarudi nyuma. Huwezi amini nilimfuata mwenyewe pale kitandani huku nikilia machozi ya kukatishwa utamu, nikitaka aendelee kunipiga deki.

Unajua wanaume wengi hawawanyonyi wapenzi wao kwa kuwa wanaona kinyaa, lakini kwenye mapenzi hasa ya kupendana hadi kushibana, hakuna kitu kinachoitwa uchafu. Kwanza hata kama mpenzi wako amepakwa matope, bado utamuona mzuri tu. Nashukuru Mr X wangu aliniamini na kufanyia hivyo, japokuwa sikuwa mgeni kwenye hayo mambo lakini kiukweli kila aliponifanyia hivi, niliishiwa nguvu na kutua mzigo mapema yaani kwa kunyonywa tu.


NYOO NIPE MUMEO 71

Alipomaliza,akanitanua miguu akiwa amepiga magoti na kuniingiza selebobo wake, taratibu, nikishuhudia jinsi ninavyommeza mzimamzima akaingiza na kutoka na asali iliyochuluzika kwa wingi.

Utamu ukanipanda nikaanza kutoa sauti zangu zile za mahaba, nikamuona mume wangu akinitazama macho yangu na kuniambia nina macho mazuri. Najua alikuwa ameona jinsi macho yangu makubwa meupe na kope zangu natural jinzi zilivyodondoka hapo kwenye sita kwa sita. Nikatabasamu na kutamani nijione.

Basi nikaanza sasa kufungua kitabu changu cha mauno, palepale akiwa amenimanua nikaanza kumnyongea taratibu, halafu nikawa naongeza spidi huku nikimuangalia alivyokuwa akitweta. Tena alifikia wakati akaniambia anapenda nilivyokuwa nafanya niendelee.

Nikawa nampa vyote na yeye akiwa ametulia tu macho yake yakiangalia kiuno changu hasa ule ushanga, ulivyokuwa ukiongeza ladha kiunoni kwangu. Tena kadri nilivyokuwa nikikatika ule ushanga ulivyokuwa ukinitekenya ulizidi kunipa hamasa ya kuendelea na kukuna nazi hadi nimtoe Mr X tui zito.

Nikajituma mtoto wa kike, kichwani nikiwa nimemuweka Fatuma, Hadija, Gululi na Kungwi, nikiiba kila kitu nilichokuwa nakijua au kukisikia kutoka kwao.

Huyu hapa Mr X alianza kupiga kelele, jambo ambalo sikuwahi kumuona akifanya, akashindwa kujizuia, akajinyoosha na kuniweka kifo cha mende huku akihema kwa nguvu, makelele yake yakabadilika na kuwa kama vile mtu amebanwa na kiazi au amekumbwa na kifafa maana alinishikilia kwa nguvu mno huku akinishindua basi hapohapo na mimi nikamnyongea ndani kwa ndani na kumbana.

Sijui ni kwa utamu au ni nini maana alining’ata hapa begani hadi nikawa naumia, uzuri mbio zake ziliishia sekunde chache tena akitetemeka na kunywea kama puto la shilingi hamsini lililotua kwenye mwiba na kuishiwa upepo.

Nilisikia michirizi ya motoo ikinimwagikia kwa ndani,nikawa nampigapiga mgongoni nikimpa pole kwa kazi kubwa aliyoifanya. Akashindwa kuitikia zaidi akiguna tu “mh! Mh!”

Kimoyomoyo nikasema: “na bado ndiyo kwanza nimeanza mafunzo ngoja nimalize.”

Itaendelea..


NYOO NIPE MUMEO 72

Tulipumzika kwanza kidogo nikimpa nafasi ya kupumua maana nilijua kwa utundu niliomfanyia kwa ile raundi ya kwanza lazima aombe poo. Nilimtazama akihema taratibu naye akinitazama akiwa haaminiamini.

Najua wanaume wengi huwa na mashaka sana kwa kuona staili mpya ambazo hajazizoea kitandani. Wengi hufikiria; “umezitoa wapi?” kwa hiyo lazima uwe makini, lakini hata mimi japokuwa hakufungua mdomo kuniuliza ikabidi nimwambie tu ukweli.

“unajua mume wangu, It was you who I was suspecting of cheating me with Fatuma, I didnt know if it was my dady! (nilikuwa nimekuhisi wewe kuwa unanisaliti na Fatuma sikujua kama ni baba),” nilianza kufunguka chezea mapenzi wewe!

“Why, haven’t I ever been trustworthy? (kwa nini, sikuwahi kuaminika?)” alishangaa Mr X wangu na kuniuliza.

“sijamaanisha hivyo, baby ni kutokana na mazingira niliyokuwa nikikuona naye. Please forgive me,” niliwahi kumuomba msamaha na kumbusu, najua hata yeye mwenyewe aliniona chizi kumuwazia anatembea na mwanamke mbaya kama Fatuma. “As I was furstrated baada ya kuhisi unatembea na Fatuma nikaamua kupigania penzi langu kwa kuboresha mapenzi yetu, hivyo nilivyoondoka nyumbani siku ile nilikaa kwa Hadija usiku tu, lakini siku zote hizi mbili nilikuwa kwa Kungwi aliyenifundisha haya yote,” nilifunguka.

“Kungwi! whats that?” aliniuliza Mr X nyusi zake zikipanda juu kwa mshangao.

“Kungwi ni mwalimu wa kiasili wa mapenzi hasa kwa wasichana,” nilimfafanulia, akaanza kuniuliza maswali kibao kiasi kwamba nilianza kumhadithia kazi za kungwi na mambo gani yafundishwa huko mkoleni.

Akaonekana kuvutiwa sana na huo utaratibu wa kuwafunda wasichana kabla ya kuingia kwenye ulimwengu wa mapenzi, akashangaa kumbe Tanzania kuna mambo mazuri kiasi hicho.



Tena mwenyewe alikiri kuona nimebadilika sana kitandani, kwanza kwa mkwara sikujipulizia marashi ya aina yoyote zaidi ya harufu ya udi niliojifukiza tangu nilivyotoka kwa Kungwi wangu. “I want to show something else you ready! (nataka kukuonesha kitu kingine upo tayari!” nilimwambia Mr X akaniambia yupo tayari basi niikamchukua bakari-kichwa wake aliyesinzia na kuanza kumpitisha kwenye ngozi ya paja langu laini kama vile nanoa kisu. Huwezi amini njia hii ya kuamsha dyudyu iliyolala baada ya cha kwanza, nilijifunza zamani sana enzi zile za darasa la Mr X part One.

Kwa sekunde chache tu niliona mlingoti ukineema, basi nikaupandia kwa juu nikageukia ukutani huku yeye nikimuachia mgogo. Staili hiyo kule Marekani wanaitaga Reverse Cowgirl ukiacha ile Cowgirl ya kawaida ambayo mimi ningegeuka na kumtazama yeye, lakini hiyo ilikuwa kinyume chake.

Basi nikamshikilia miguu na kuanza kuimeza mashine yake robo, nusu na ikaingia yooote. Sasa hapo ndo nilitaka kumuonesha ule ufundi wa kunyanyua tako moja kiasi kwamba hata kama akisikia kwa Fatuma aone hakuna jipya.

Niligeuka na kumtazama Mr X aliyelala akisikilizia kitu gani nataka kufanya, na mimi wala sikuwa na haraka maana kuku wangu mwenyewe kwanini nimvizie na mawe?

Nikaanza kupanda juu taratibu na kunyanyukia kama vile naendesha baskeli, halafu utamu ulipokolea nilistop ghafla na kuanza kunyanyua tako moja juu kisha nikapandisha jingine, halafu nikaendelea na viuno mgandisho ambavyo najua hakuwahi kuviona. Nikarudia tena na tena, nilijua fika kwa kuwa alikuwa akiniangalia kwa nyuma yaani mgogoni, aliweza kuniona vizuri sehemu zangu za nyuma zikitikisika.


NYOO NIPE MUMEO 74

Huwezi amini siku hiyo ndiyo nilijua kuwa wanaume wanachanganywa sana na macho yao tu, maana kwa mtindo wa kumchezeshea tako tu, Mr X wangu hakuchukua hata dakika mbili. Nilianza kumuona akinishikilia kama anataka kudandia ukuta. Akanimwagia kwa mara ya pili.

Sikutaka kumchosha sana. Tukaenda kuoga na kurudi kitandani, tuliporudi tu Mr X alizidi kunisifia na kuniambia anajihisi kila saa mashine yake ikimsisimka kwa utamu niliompa, nikafananisha maneno hayo na yale aliyosema Steve baada ya kutembea na Fatuma. Nikajiuliza ina maana hata baba naye anajisikia hivyohivyo au?

Ina maana kumbe mwanaume akiridhishwa kiwango cha mwisho anakuwa anajisikiaga hivyo eeh? @Charles13jr @kinambari @masoud_k_k

“Mke wangu kama ndiyo umefundishwa hayo mambo, basi inabidi uwe unaenda kujifunza zaidi, lakini nataka uwe unatokea nyumbani, sitaki tutengane tena,” alisema Mr X nikaona kweli amekolea.

Huwezi amini wakati tumelala pale hotelini, katikati ya usiku akaniamsha na kuniomba tena, maana alisema hawezi kulala, nikampa cha kiuvivu alipomaliza haja zake akanifuta kwa kanga niliyobeba na kulala pembeni yangu, lakini alichonishangaza akaichomeka nanihii yake tena ndani ya kipapatilo changu eti akisema anatamani nilale nayo ikiwa ndani.

Nikafurahia moyoni kuwa kweli leo Mr X nimempata, basi na mimi nikalala na pipi yangu mdomoni.

Raha siyo rahaaa!?

Itaendelea…


NYOO NIPE MUMEO 75

Asubuhi mapema mno tukiwa tumeoga safi,tulienda kwenye restaurant ya ile hoteli tuliyolala na kufungua kinywa, mume wangu akaagiza Capuccino na mimi nikaamua tu kunywa maziwa na kuchanganya na kahawa safi.

Tulirudi nyumbani tukiwa tumeshikana mikono na Mr X wangu kwa mapenzi mazito kiasi kwamba hata mama alipotuangalia alijisikia faraja.

Ama kweli Mungu kaumba watu, japokuwa mama alikuwa na msogo wa mawazo yake kuhusu baba lakini aliweza kuficha majonzi yake vyema ndani ya vungu za moyo wake na kututazama kwa tabasamu kama vile hakuna kitu kinachomsibu.

Nikawa nastaajabu kuna wanawake wangapi duniani wana moyo wa upendo na uvumilivu kiasi hicho lakini wanaume hawawathamini na zaidi wanawatesa kila uchwao.

Sikuweza kuendelea kumshika mkono Mr X kwa kuwa nilijisikia vibaya, maana siwezi kuonesha mahaba yangu mbele ya mama ambaye ndo kwanza mapenzi anayasikilizia bombani.

Angekuwa kijana kama mimi ningempeleka kwa Bi Gululi ili naye akafundwe, lakini kwa kuwa umri wake ulikuwa umeenda, kulikuwa hakuna cha kukiokoa, nikamuachia mwenyewe aendelee na maombi yake maana kila mara hujifungia ndani kwake akisali rozali.

“Siwezi kukaa tu hivi lazima nimsaidie mama,” nilisema nikimwambia Mr X baada ya kumpokea Kendrick kutoka kwa dada.

“unataka kumsaidia kivipi?” alihoji Jermaine.

“kama baba kweli haoni wala hasikii kwa Fatuma, cha kwanza kabisa, sitaki umpe baba hela yoyote, nataka hela zote kuanzia mahali yangu zipitie kwa mama, najua akikosa hela za kuhonga, penzi lake na Fatuma ndiyo litakuwa mwisho,” nilisema.

“hapana Mary, wewe unaongea tu lakini mimi mwanaume; anapokuja baba yako kuniomba hela ya kununua nguo nitaanzaje kumnyima?” aliuliza Mr X nikaona kweli kwa mkwe kumnyima ni ngumu, natakiwa kufikiria cha kufanya tena nifanye haraka mno.

Wakati huo baba alikuwa ndo anatoka kuamka, alipotuona alitabasamu na kujaribu kuongea na Jermaine kwa kiingereza chake cha shule ya Mkoloni.


NYOO NIPE MUMEO 76

“Hallow Mr Jermaine. Me is seeing you there. Is the morning great! Is’nt it” aliongea kwa kuungaunga, basi mimi kuona tu sura yake alikuwa ameshanitumbukia nyongo, nikaamua kuingia zangu ndani na mwanangu.

Kichwani nikiwaza nitamkomoaje baba, na huyo Fatuma wake ili waachane? Sikupata jibu.

Ilipofika mchana hivi wakati tunaandaa chakula, mimi nikatoa wazo kwa wenzangu kuwa tungeenda familia nzima ufukweni kubarizi, na hasa kumtembeza mama ambaye alizoea tu kukaa nyumbani.

Wazo hilo likaonekana kufurahiwa mno hasa na dada yangu Mage, basi mida ya saa tisa tu, tulikodi taksi na kuondoka zetu tukielekea Kawe, tukiitafuta bichi ya Piccolo Hoteli.

Tulitulia hapo huku kila mtu akivinjari kwa mtindo wake, mimi vile ninavyoyapenda maji, nilirukia kwenye swimming pool na nguo zangu za kuongelea nikawa nashindana na dada nani atamshinda mwenzake kufika kulee na kurudi huku mwanzo.

Tukawa tunaenda mwanzo hadi mwisho, lakini kote huko mimi nikiibuka kidedea. Mchezo mzima ukawa unaboa maana kila saa nilishinda mimi tu. Basi tukapiga mapicha ya kutosha, nyingine nikaomba dada Mage anipige nikiwa nimebebwa na mume wangu na mapozi kibao ya aina hiyo.

Palepale sikukawiza nikabadilisha dp yangu ya Whatsapp na kuweka picha yangu na Mr X tukiwa penzi penzini nikaandika status, “Forever and a day”.

Huwezi amini dakika mbili nyingi, nikapokea ujumbe kutoka kwa Hadija; “Mh shoga mmeenda bichi hata kuniambia na mimi nije?” Nilijua nia yake, nikamtumia meseji nikimwambia; “shoga ni mtoko wa kifamilia nitakushtua siku nyingine,” basi najua ilimgusa kweli maana alifyata kimya.

Dakika chache baadaye niliona simu ya Gululi pia ikiingia, nikapokea; “hallow shoga, mambo?”

“poa tu za tangu jana!”


NYOO NIPE MUMEO 77

“safi.. nia ya kukupigia shoga yangu, kama nilivyokwambia huyu Hadija siyo mtu mzuri hata kidogo, hapa ninavyokupigia, jana wewe unatoka mwenzako Hadija anaingia. sasa unajua alichokifanya?” alisema Gululi akiniuliza swali lisilo la msingi, maana yeye ndiye aliyejua alichokifanya Hadija, sasa ananiuliza mimi nitajuaje sasa!

“amefanyaje?”niliuliza kwa utulivu nikijitahidi kushusha shauku yangu “alipokuja alianza kuniomba nimuelekeze tena jinsi ya kuangalia majina kwenye simu, akaingiza namba yako kabisa, tena akaangalia jina lako kwa siri niliona limeandikwa Mary Geofrey, si ni jina lako?” alisema Gululi moyo wangu ukianza kupiga kwa kasi.

“ndio ni jina langu?” niliitikia kwa hofu, wakati huo mume wangu alinisogelea na kuniuliza kulikoni maana nilionekana kujaa mashaka. Nikajichekesha kama vile hamna kitu, alipoondoka nikaweka simu sikioni tena.

“kwa hiyo unadhani anaenda kuniroga kwa mganga si ndiyo?” “ndiyo ninavyokwambia shoga yangu, mwanzoni alichukua la mumeo, sasa hivi jina lako. Sasa hayo tisa kumi ni kwamba, wakati nimeenda kuoga, shoga yule si alikuwa akilipekua begi lako la nguo, sasa kama kuna kitu ulikiweka hovyo shoga njoo ukiangalie asije akawa amekuibia.

“haya usijali nitakuja kesho,” nilimjibu Gululi kwa utulivu kana kwamba sikuwa naogopa chochote kumbe alikuwa amenivuruga mno. Ile raha ya kurukaruka tena ufukweni iliisha. Giza lilipoingia tulirudi zetu nyumbani.

Kesho yake mapema nikamuaga mume wangu kuwa naenda kwa kungwi, akanipa baraka zote.

Nilipofika tu, Gululi akanipokea kwa nguvu zote, japo kuwa alinieleza umbea wote jana lakini akaurudia tena siku hiyo, nikaingia harakaharaka kuangalia kwenye begi langu kama kuna kitu gani ambacho Hadija alikuwa akikitafuta.

Katika kupekuapekua nikashangaa chupi yangu moja siioni, nikamuuliza Gululi kama pengine aliiona nimeianika na kusahau, lakini alikataa katakata.

“we Mary! Au ndiyo Hadija ameichukua! Mama yangu kweli yule ameenda nayo kwa mganga na inaonekana hilo dudu analolitengeneza siyo mchezo! shoga jiandae,” alisema Gululi, nikazidi kuogopa


MWISHOOO


0 comments:

Post a Comment

BLOG