Search This Blog

Monday, January 24, 2022

MCHEPUKO WA ZANZIBAR - 3

   

Chombezo : Mchepuko Wa Zanzibar

Sehemu Ya Tatu (3)


“ndiyo tena ni gwiji, anaogopwa hapa,”

“mimi simuogopi!” alisema Damian.



Kama kawaida asubuhi na mchana haikuwa ya kusisimua kwa kina Bushiri na Damian. Wateja walewale wanaume walifika na kuondoka.

Wakati jua likizama na wavuvi kuondoka zako baharini, wakina Damian na Bushiri wakachekelea; wakawasha kandili zao, kutia mtego wake za watu.

Sasa kumbe taarifa zilifika mbali kwenye kingo zote za kijiji kuwa kuna duka na marikiti ndogo ya usiku, basi wateja wakamiminika kuliko jana yake, wote wakiwa wakike.

“nipatie sukari guru na iriki,” alisema mdada Fulani wa kipemba, pua yake ikiwa imechongoa mno na macho yake kuingia ndani sana hiyo ikimfanya awe na sura ya usiriaz mno, lakini weupe wake na urefu ulimchanganya Bushiri.

Wakati Damian akimpatia mteja wake huyo vitu hivyo na kurudisha chenji ya senti kadhaa, Bushiri akatia neno: “Zamda, njoo na huku nikupatie tangawizi, ukaponde chai murua!”

“mie siyo Zamda, naitwa Najma,” alisema binti huyo.

“ooh nimekisia tu maana uzuri wako nilijua lazima tu jina lako likawe na irabu ‘a’ ndani yake; kwa hiyo Najma, upikapo chai utujalie na sie japo vikombe viwili tu, maana baridi ati!” alizidi kuchombeza Bushiri, Damian akamshangaa mwenzake akiona jinsi alivyo fundi wa maneno.

“mh, aya tukijaliwa,” alisema huyo Zamda akiondoka zake.

“Damian huyu akileta chai tu lazima nimkae, leoleo,” aliongea Bushiri shetani akiwa amempanda kabisa kichwani.

“sasa utamfanyia wapi usiku huu? Utafunga genge?” aliuliza Damian.

“wee huoni mikoko hiyo? Sifungi, dakika kumi tu narejea,” alisema Bushiri akionesha msitu wa mikoko kwenye upwa wa bahari iliyotanda hatua chache nyuma yao.

Basi, wakafika wateja wengine wengi na kila mmoja wao, Bushiri alitupia kaneno kake. Mara wakafika wale wasichana wa jana yake; Habiba na Shahida.

“habari zenu wakaka?” walisalimia kwa pamoja.

“salama tu, karibuni,” aliitikia Damian, Bushiri akamuita mmoja pembeni yule mrefu mkubwa, Shahida. Maana ugonjwa wake ni wasichana warefu tu. Yuenda mkewe alikuwa mfupi ndiyo maana shetani lake la kuchepuka lilikuwa na kiu na warefu.


“Damwan, mie nna shida!” alisema Habiba akijilegeza.

“shida gani?” aliuliza Damian japo alichukia jina lake kukosewa.

“nataka leso, lakini bwana wangu hajaniachia hela, hadi arudi baharini kesho nitakueletea!”

“mh Habiba, mimi sikopeshi mbona!”

“we Damwan, mwenzio tumbo lanisumbua nipo mwezini mwenzio, nitafanyaje na sina khanga kongwe nyumbani,” alilalamika Habiba.

“we, hizi leso zinaletwa kutoka Dubai, na hapo mzigo kuupata mjini ni tabu sana, nitakukopeshaje kirahisi hivyo! Labda tuandikishiane!” alisema Damian akitoa daftari.

“mh we bahiri,” alisema Habiba na kulazimika kuandika jina na deni analodaiwa. Damian akatoa leso na kumpatia Habiba. “Damian niangalizie!” alisema Bushiri akimwambia Damian wakati huo akilikokotaza zigo lake kuelekea nalo mikokoni. Looh rahisi kiasi hicho! Aliwaza Damian akivurugwa na yeye akili zikamruka akamtazama Habiba.

“Habiba, utamaliza lini mwezi wako, twende walikoenda Bushiri na dada ako!?”

“mh kwani wewe unataka?”

“ndiyo, nataka, sijafanya tangu nije huku!” aliyesema si Damian bali kichwa cha chini kiliuteka mdomo saa hiyo.

“wee pole, hapo una ashki balaa!?”

“ndiyo nyege au?”

“ndiyo,”

“ndiyo,”

“basi nikunyonye leo, halafu nikipona nitakupa unifanye, unisamehe deni la leso,” alisema Habiba.

“uninyonyeje?”

“we hujawahi kunyonywa huko?”

“sijawahi, ninyonye njoo, usinitie meno tu!” alisema Damian akifungua duka kabisa.

Habiba akaingia ndani ya kiduka akakalia boksi na kumvua suruali Damian, akakuta Nkurunzinza ameshasimama kukataa kutoka madarakani. “Doh Damwan una kubwa! nipe na pipi kifua,” alisema Habiba.

“utalipia?”

“kha, we bahiri hutaki utamu?”

“basi chukua hii hapa,” alisema Damian wa watu.

Habiba akalimung’unyia na pipi kifua, dohhhh, Damian akawa kama amebanwa na kiazi. Akayumbayumba kwa utamu.

“we kaka una sinzia au? dukani!” alisema si mwingine bali ni Mama Aymar, Naifathy, mke wa mzee Salum bin Salum, mwanamke aliyemtikisa moyo Damian. Uzuri kwa nje Damian alionekana kuanzia kifuani hivyo yaliyoendelea kwa chini hakuna aliyejua isipokuwa yeye tu na Habiba eliyeendelea kama kawaida. “uuuu, uuna taka nikusaiii, diiiii, eee, nini?” alizungumza kwa vituo visivyostahiki maana chini alikokonwa htr



“Naomba ngano na hamira,” alisema Naifathy, Damian likampitia huku na kutokea huku maana ubaridi wa pipi kifua; msuguo wa ulimi, mibano ya midomo na min’gato dhaifu ya meno ya Habiba yalimfikisha shindo lake, akasaga juisi na kuyamwaga mashudu ya haja.

Akahema huku juujuu akitamka: “haaaaaa, haaaa!” angali amefumba macho kwa ugiligili.

“wee, nimekwambia Hamira, huijui kuitamka au! Mbona waishia haaa! Haa! Kama wataka kunimeza mie!?” alifoka Naifathy.

Sasa akili za Damian zilirudi akachomoka mikononi mwa Habiba aliyekuwa chini huko akijifuta udelele na kutulia kimya akisubiri huyo mteja aondoke zake kwanza.

Haraka Damian akapima ngano robo na kumpatia Naifathy na kuchukua hela yake asiseme neno maana mfumo wake wa fahamu bado ulikuwa ukikata mawasiliano na kichwa cha chini na kurudisha kwenye kichwa cha juu.

“mh leo una usingizi waonekana, mbona chenji waniongezea!?” alisema Naifathy akirudi maana alishapiga hatua chache mbele.

“nilikupa senti mbili, unanipaje senti moja badala ya thumuni, wanihonga?”

“aisee, nilikuwa nimechanganyikiwa samahani,”

“mh, nimekuchanganya eeh kwa uzuri wangu kalaghabao,” alisema Naifathy akiondoka huku akitikisa na kutazama nyuma kila mara kumuangalia Damian.

Basi Habiba akasimama na kutoka nje ya duka, akachukua maji pale nje kwenye ndoo na kusukutua mdomo kisha akasimama mbele ya Damian.

“mh we mwanaume, umejaliwa, laiti nisingekuwa mwezini leo ningekuonja walahi! Nikimaliza tu nakuja, sitaki umpe mwingine kwanza kabla yangu maana nilishaanza ona inzi wengi,” alisema Habiba akiwa nusu siriaz nusu utani tena huku akikitazama kinjia alichoendea Naifathy na kumgeukia Damian tena.

“Sikia, yule aliyetoka hapa ni Naifathy kama humjui! ana hamu nyingi yule. Mumewe anamuoa leo, wiki ijayo anaishiwa nguvu za kupanda mtungi, yaani hajafaidishwa hata kidogo, ashukuru tu aliolewa na mimba ndiyo huyo mtoto wake anamsitiri. Naona anajipendekeza kwako kuwa makini mumewe anamchunga nasikia kamtilia na dawa ukimlala unapata dhara,” alisema Habiba nyakati hizo ndiyo Shahida naye alitoka vichakani na Bushiri.



Bushiri akionekana mwepesii! Akafika na kuchukua fumbate la nyanya, kitunguu maji na pilipili akamfungia Shahida kwenye galazeti na kumpatia.

“hizo zawadi yako,” alisema Bushiri. “asante Bushiri, bora wee sio bahiri kama Damwani,” alitia za hivyo Habiba kumuumiza roho Damian.

Haoo wakaondoka zao.

Damian akisikia afueni ambayo hakuwahi kuipata mihula mingi. Alisikia damu yake ikizunguka kawaida sasa na hata alifikiria sawasawa, akaanza kufunga duka lake maana ilikuwa saa nne usiku hiyo.

Akatazama mahesabu ya siku kichwa chake kikifanya kazi harakaharaka, akatazama bidhaa zilizobaki na zilizopungua akashtuka kuona chupio zimetoweka pale chini.

“mshenzi Habiba ameniibia!” alisema kwa sauti Damian.

“Habiba? Ameibaje? Ulikuwa naye dukani?” aliuliza Bushiri maswali mengi harakaharaka naye akaacha hata kutandika gunia juu ya vitunguu.

“agh aliingia dukani, alikuwa akininyonya babu,” alisema Damian.

“weee mbona mimi sijawahi kufanywa hivyo, aisee itabidi uniachie Habiba anionjeshe utamu huo,” aliongea Bushiri kwa tamaa kabisa yaani.

“we subiri kwanza namdai, hadi alipie deni langu, nikimmaliza we mchukue tu, mimi simtaki,” alijibu Damian, akili yake ikirudi upya kichwani akimuwaza Naifathy na alichosikia kutoka kwa Habiba kuwa hajaguswa muda ndiyo kilimchanganya akili.

Basi wakafunga na kuondoka njia nzima Bushiri akimueleza Damian alivyofanya na Shahida kwenye vichaka kuanzia jinsi walivyosimama akishikia mashina ya mikoko huku wakiswaga mbuzi na kupara samaki.

“aisee, we yule mtoto mtamu,” alisema Bushiri, Damian akajaa wivu mno.

Wakafikia njia panda na Damian akaelekea kwake, akakuta kama kawaida jumba limepigwa kufuri, akagonga mno lakini mlango haukufunguliwa, akapiga hesabu na kuona njia nzuri ni kutembea hadi usawa wa dirisha la Sabrina na kumuita.

“Sabrina, sabrinaa!”

“abeeeee!” “naomba nifungulie, mimi Damian.”

Baada ya dakika chache, mlango ukafunguliwa na Sabrina mtoto mlaini nywele hadi mgongoni. Alionekana anausingizi bado na alianza kurejea chumbani kwake.

“Sabrina, asante, chukua na hii,” alisema Damian akimpa jojo mbili Sabrina kama bahshishi ya kumfungulia mlango siku hiyo. Sabrina akasema asante yake na kwenda kulala.




Siku hiyo tena ilikuwa ni ya Damian kudamka asubuhi na kwenda dukani kwake, lakini akaona afagie kwanza uwanja na kudeki chooni maana mara kadhaa akiwa amewahi mno hufanya hivyo. Akaanza kudeki chooni na bafuni kisha akashika ufagio kuanza kufagia uwanja.

Ndiyo akaona mlango wa chumba cha Sabrina ukifunguka na Sabrina akitoka mle ndani akifikicha macho maana bado ilikuwa ni mapambazuko.

“salamaleko,” alisalimia Damian.

“aleykum Salaam,” aliitikia vizuri Sabrina.

“he, kaka niache tu nifagie mie,” alisema Sabrina.

“hapana we niache tu ninamaliza fastafasta tu hapa,” “hapana mama atanikaripia, amesema nihakikishe haushiki mfagio wowote, tena amesema kama ukiwa na nguo chafu nikufulie,” alisema Sabrina akikwapua ufagio kutoka kwa Damian na kuendelea yeye kufagia.

“aaar, eee, aisee nguo ninazo kweli lakini nafuaga mwenyewe jumapili,” “hapana mama atanichapa, alisema nikwambie maana majirani na wapangaji hukushangaa ukifua.”

“haa! Kwanini wanishangae nikifua?” aliuliza Damian.

“mwanaume mwenye ndevu hafui, lah!” alifafanua nikavuta picha na kuona ni kweli sikuwahi kumuona mwanaume anafua tangu nifike Jambiani na nilikuwa mimi tu kwa kweli.

“Kwani bara wanaume wafua?”

“ndiyo, tunafua, tunapika, tunafagia na tunafanya kila kitu hata kubeba watoto mgongoni,”

“mh, wanawake wenu wa huko wana raha!?” alisema Sabrina kumbe naye ni mwingi wa maneno sema sikuwahi kuzungumza naye kama siku hiyo.

“hahaa,” nilitupia cheko nikiwa nakinga maji kwenye ndoo ili nikaoge.


ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

BLOG