Search This Blog

Monday, January 24, 2022

KITUNGUU SAUMU - 3

   

Chombezo : Kitunguu Saumu

Sehemu Ya Tatu (3)


KITUNGUU SAUMU 23

“Mh kweli lakini sasa nitafanyaje!” alisema Naima akihuzunika.

“oooh usisononeke, Naima, nimekupima moyo wako, mwingine angesema nitakupa hela, lakini wewe unaonekana haupo hivyo, unaonekana unataka kujifunza zaidi, nitakufundisha lakini naomba uwe msiri na hata utakapofika kuwafundisha hao Wazungu, weka ziada, usiyatoe yote, umesikia!” alisihi Kungwi, uso wa Naima ukapata nuru, akatabasamu tena akifurahia kuridhiwa na Kungwi.

Wakaagana kwa maana Kungwi aliwahi darasa lake la urembo maana asubuhi alitoka kufundisha darasa lake la mapishi na usiku ana mkole wa mtandaoni kwa magrupu ya whatsapp, sasa utashangaa hilo darasa la tiba analifanyiaga wapi? Doh alikuwa bize huyo.

Wakati Ilham anaondoka na Naima anatuliza nafsi yake, Friday aliingia akionekana ametoka kuongea na Ilham kwa kina huko nje.

“ Enhee sasa sikia, asingekuwa kungwi ningekurudisha kwenu kumbe umezaa!?” alikoroma Friday.

“kuzaa ndiyo nini?” alijibu Naima.

“maana yake una michirizi ya tumbo, huko chini hakuna ladha tena, maziwa yamelala na hiyo yote ni kuharibiana tu dili dah! lakini lazima ujiongezage na wewe mwenyewe bwana, ulikuwa unaishije bila kujua hata kitu kimoja?!” alikoroma Friday.

Doh Naima akainuka akitetemeka, akaanza kuvua nguo zake zote na kubakia mtupu mbele ya Friday.

“Unanisema sana, haya niangalie maziwa, niangalie hiyo michirizi unayoidai! Niingize kabisa upime kama nimepelepweta! Hii safari yenyewe naona ni mikosi tu, ukitaka sema niondoke nitaondoka! Sio kunisema tu kila saa!” alisema kwa hasira Naima huku akilia.

Doh! Friday, kwa aibu akamtazama Naima alivyokuwa na shepu nzuri, alikuwa na ngozi nyeusi ya kung’ara, alikuwa akiita; kifua chake kama hajazaa. Kweli Naima alikuwa mzuri wa sura na figa lakini alikuwa na michirizi ndiyo, hasa tumboni na Hii ndiyo iliyomtia shaka Friday.

Lakini ameshaingia choo cha kike hakuna namna, akaokota shuka pale kitandani na kumfunika Naima kisha akamkumbatia akimuomba msamaha, maana paka ukimbana sana na kumnyima uhuru lazima atakuparua na ndiyo ilivyokuwa kwa Naima, alikubali kuwa hajui, alipambana kujua, lakini ukimkatisha tamaa, atakurarua na hapo alimuonesha makucha tu Friday.


KITUNGUU SAUMU 24

“Samahani Naima, kuanzia leo tutakuwa pamoja tutasaidiana hata tukiwa huko Marekani, usichokijua nitakufundisha na sitakusema tena vibaya, kitu kingine tukifika huko tafadhali jina lako ni Adellah!” alisema Friday na kumbusu Naima shavuni huku akiendelea kumpapasa mgongoni.

Naima hasira zikatulia akapoa na kukaa kitandani. Taratibu wakaanza kuzungumza mengi na kuwa marafiki, tena wakapiga stori za huko Marekani na kumbe hata Friday hakuwahi kwenda na yeye ilikuwa mara yake ya kwanza.

Usiku ule hawakulala kwa shauku, kila mmoja alihofia asije kupitiliza muda wa ndege, wakajihimu saa kumi alfajiri wakapelekwa na usafiri wa hoteli hadi uwanja wa ndege. Wakadandia ndege yao na saa kumi na mbili kamili wakapaa mawinguni.

Ilitisha kuona ardhi ikiachwa na kupaa ndani ya mashine tu, hapo ndiyo pa kusali sala zote;lakini presha na wasiwasi huisha pale unapozoea, tena ikiwa safari ndefu kama hiyo. Basi ikawa Naima na Friday wakapitiwa na usingizi kwa kuwa hawakulala usiku wa kuamkia siku hiyo.

Naima alilala lakini alihofia asije kushtuka akajikuta yupo Tanzania kwenye magheto ya Tandika huko na yote hayo yawe ni ndoto. Lakini Lah! alishtuka na kujikuta akiwa ndani ya ndege tena, ilikuwa ni furaha iliyoje.

Baaada ya safari ndefu sasa walifika Alabama uwanja wa ndege wa Birmingham-Shuttlesworth usiku wa manane, kulikuwa na baridi kama la Lushoto, ilikuwa ni bonge la uwanja na kila kitu kilikuwa kikubwa mara nne ya Tanzania, kasoro tu watu.

Basi na ushamba wao, wakatoka uwanja wa ndege na pale kwa kutokea wakashangaa kuona umati mkubwa wa wazungu waume kwa wanawake ambao walipowaona tu walipiga makelele wakiita: Fridayyyyyy! Adellahhhhhhh!”

Mama Yangu Naima akaogopa, hakuwahi kuona wazungu wengi hivyo wakiwashobokea, tena zaidi ya hamsini wengine wakiwa na kamera za video kabisa. Naima akamshikilia Friday kwa hofu. “Acha ujinga niige mimi!” alisema Friday akipunga mkono na kuachia tabasamu pana, na yeye Naima akafanya hivyohivyo.

Itaendelea..


KITUNGUU SAUMU 25

Ilikuwa ni umati kabisa; wakina mama na akina baba wa kizungu wakiwawaoh wakina Naima na Friday na kuwapatia maua ya aina mbalimbali. Ulikuwa ni upendo mkubwa waliooneshwa.

Basi kubwa liliwachukua hapo na kuwapeleka huko waendako, humo kwenye gari, wazungu wakiwauliza maswali akina Naima wakiwaongelesha na kuwafurahisha kwa kila neno, Naima yeye akawa akiiga ya Friday tu akatabasamu na neno kubwa aliloongea ni Thank you, na Amazing!

Baada ya safari ya mwendo kidogo gari lilitoka barabara ya mji na kuingia kwenye barabara inayopita kwenye pori jepesi kisha wakatokea kwenye jumba kubwa lilozungukwa na kuta kuukuu. Wakaingia ndani na kushuka.

“we are so grateful that you’ve managed to come, ooh I’m, Mr Howard Johnson!” aliongea mwanaume Fulani wa makamo, akiwasalimia akina Naima na Friday huku wakisaidia kuchukua mabegi yao kuyaingiza huko kwenye hilo kasri.

“Ooh that’s so nice of you, Mr Howard, we so happy to be here! Gosh so many people!” alitiririka Friday, Naima akawa anatumbua tu macho pengine akijutia kwanini hakujifunza ngeli.

Mara mbele yao akatokea mwana mama mmoja mtu mzima, mwenye pua ndefu na macho makali, mashavu yake yalikuwa yamejaa kuonesha kuwa alikuwa mcheshi lakini pia ni siriaz kwenye kazi, pembeni yake akiwa na msichana wa kike wa asili ya Kiafrika.

“huyo ndiyo Madam Alexandrina“ alisema Friday akimnong’oneza Naima, aliyegangamala kiheshima zaidi.

“ooh Friday come gimme a hug!” alisema Madam Alexadrina, Friday akatabasamu na kumkumbatia.

“Oooh Adellah! I presume;” alisema Madam.. akimgeukia Naima, Naima asijue neno alilosema mama huyo akatabasamu na kutaka kusema: Thank You! Loh aliyemuokoa alikuwa ni huyo msichana wa kiafrika hapo pembeni aliyesema: “Madam anasema,bila shaka wewe ndiyo Adellah;”

“Yah …Yess..Ndiyo!” alijibu harakaharaka Naima naye akakumbatiana na Madam Alex na kuingizwa ndani wakikaribishwa vyumba vyao wajiandae tena kuna wafanyakazi wakawekwa kuwasaidia kama watahitaji msaada wowote.

Loh! Naima sasa ndiyo akaona usiriaz wa hilo dili, unaambiwa tumbo la woga lilimshika kila alipofikiria majukumu yake.


KITUNGUU SAUMU 26

Akaingia kuoga maji ya moto, kwenye bafu la kisasa, tena ndani ya vyumba kulikuwa na air condition spesho za kutema joto lililosaidia kustahimili baridi, akatoka na kuvaa vazi jipya na kujishindilia na pullover maana waliambiwa saa chache washuke hapo chini kupata mlo wa usiku na kutambulishwa kwa wanafunzi wao.

Kweli walipochukuliwa na kushushwa hapo kwenye sebule kuukuu. walikuta meza kubwa mno juu ina kila aina ya chakula kilichowekwa hapo mezani na mvinyo mwekundu ukimiminwa kwenye glasi zilizowekwa sanjari na kila kiti.

Ule umati mzima ulikuwepo hapo na macho ya kila mmoja yalikuwa kwa Friday na Naima tu. Vuta picha.

“Ladies and Gentlemen, as I promised; I brought to you these special guests all the way from Tanzania, just to teach us about their native ways of doing sex, I know we have questions and we are so eager to learn, but not today please we have to let them rest we will start tomorrow, but lets hear a little from them!” alisema Madam Alex. Wazungu wakashangilia na kumtazama Naima na Friday.

“Oh Madam anasema nyie ni wageni kutoka Tanzania mmekuja kufundisha jinsi ya kufanya mapenzi kiasili kuanzia kesho, anataka muwatoe shauku wenyeji kwa kusema neno kidogo,” alisema Yule dada wa kiafrika akimwambia Naima, Loh Naima akaelewa sasa.

“sisi ni makungwi, tumeleta mambo mengi ya kiasili ya jinsi mapenzi yanavyofanyika kwetu, tumeyajumuisha masomo yetu katika matawi makuu manne, la kwanza, urembo/usafi; mapishi, mapenzi na tiba ya baadhi ya magonjwa au matatizo yanayohusiana na mapenzi na matawi yote hayo mtaona yanahusiana, tukutane kesho!” alisema Naima kwa Kiswahili akiyakopi maneno yaleyale ya Kungwi wa Kiarabu aliyoambiwaga akiwa Dar, akijitutumua na kujiongeza, hakutaka Friday amuone kazubaa.

Wakati huo Yule mdada akatafsiri kwa kiingereza, wazungu wakapiga makelele wakifurahia tena wakagonga na glasi kabisa wakiwafurahia Naima na Friday, Friday akamtazama Naima akitabasamu na kumuoneshea ishara ya dole.

Je, unataka kuingia katika darasa la kungwi kuanzia kesho?

USIKOSE DARASA LA MAFUNZO YA SIKU TANO; YA MATAWI MANNE YA UNYAGO WA KUNGWI WA KIARABU MWENYEWE KWA BEI YA SHILINGI 5,000/ TU! KWA SIKU MOJA NI SHILINGI 1,000/ NI KWA WANAWAKE TU WALIOZIDI UMRI WA MIAKA 18. MADA NI NNE KWA SIKU. LIPIA KUPITIA # USHAURI BINAFSI NI BURE KWA WANADARASA TU.

Itaendelea..


KITUNGUU SAUMU 27

Wakati walipomaliza kula ndipo Naima akajihusianisha na yule msichana aliyekuwa akikifahamu Kiswahili, akagundua aliitwa Jenny, akamuomba ampatie laini mpya ya simu na bundle za internet.

Ndipo akaambiwa kuwa kumbe Marekani hakuna shida za kujiunga na bando la internet kote kumeunganishwa bure, pengine kulipia ni bill za kupiga simu ambazo hulipwa kwa mwezi.

Naima akapatiwa alivyovihitaji kisha akaingia chumbani kwake akiwaaga wenyeji wake; kwa kusema “Goodnight every one!”

Akajifungia chumbani kwake na kutazama saa iliyoonesha kuwa ni saa tano usiku. Akapiga video call ya whatsapp kwa Ilham.

Doh kumbe Tanzania ndiyo huko ilikuwa ni saa saba mchana hivyo akapata nafasi nzuri ya kuzungumza naye; akamwambia walivyofika salama Marekani na kupokewa vizuri lakini kikubwa alitaka kufundishwa nini atakachokifundisha kwenye darasa la asubuhi ili asiyumbe.

Sasa Kungwi, aliyeonekana yupo bize nyumbani akipika akamuachia mfanyakazi wake, kisha na simu yake akaingia chumbani na kuanza kumpanga huyo mwanafunzi mpya asiyejua mambo sawasawa. Wakaongea kwa kirefu mno.

Naima alichofanya ni kutikia tu kisha walipomaliza, akakumbuka dawa alizopewa na daktari za fangasi, akatumbukiza kidonge ndani ya kishududu chake na kulala usingizi wa juujuu maana ugenini hakulaliki kistarehe.

Kwa upande wa Friday, usiku huo alikuwa na Madam Alexandrina chumbani kwake.

“you re so handsome Friday, I find myself wanting to taste that African tactics of yours! (wewe ni hendsome Friday, najikuta nikitaka sana kuonja hayo maujanja ya Kiafrika kutoka kwako); alisema Madam Alexandrina.

“hahaaa! I’m afraid you will fall in love with me, (naogopa utanipenda!)” alijibu Friday.

“I guess that will be at my own risk, but please show me that cassava, u’ve been bragged about very much” (hiyo utakuwa hasara yangu, lakini tafadhali nioneshe huo muhogo uliokuwa ukijisifu nao sana) alisema Madam Alexandrina akimsogelea Friday na kuupitisha mkono wake juu ya suruali ya Friday, akigusagusa ukubwa wa mtalimbo uliotutumuka kwa kila mguso wake ukavutika na kukaribia kufika magotini. Yaliyoendelea humo ndani ni miguno tu.

KITUNGUU SAUMU 28

Asubuhi kulikucha na baada ya shughuli zote,Naima na Friday, wakaongozwa kwenye bustani ya nyumba hiyo, huko ndiyo darasa lilipokuwepo, wazungu wa watu walijaa bustanini wakiwa wamekiketi kutazama ubao mdogo wa kusimamishwa. Ilionesha kuwa Naima na Friday walitakiwa kukaa pale mbele kama walimu na kufundisha.

Friday kichwani alikuwa amejiandaa kutambulishana na hao wanafunzi na mada ya jinsi ya kumenyana tu, hakufuata topic, lakini Naima akiwa na matirio aliyotiwa na kungwi jana yake akamuita Yule mtafsiri wake na kusimama pale ubaoni bila kuyumba.

Akawasalimia; wote wakamuitikia, lakini hasa sauti za kina baba zilikuwa juu mno.

Friday naye akasalimia, lakini sauti za kina mama zikawa juu zaidi. Doh wanawake, wanaume ni walewale tu kama bongo tu kumbe.

“Okey, naomba leo tufahamiane, naomba tujitambulishe, majina na kazi zetu ili tuzoeane kabla ya masomo,” alisema Madam Alexandrina. Akaanza yeye kujitambulisha.

“Yah alikuwa mtaalamu wa sayansi ya mapenzi, tena ni profesa kabisa, kasomea chuo. Akafuata mzee mmoja aliitwa Duncan, huyo ni mtaalamu wa saikolojia; akaja mwanamama Linda, ni mtaalamu wa sayansi ya jamii, akaja mwingine sijui nani! Yaani wote hapo walikuwa ni watu wazito tu, lakini ndio Marekani kulivyo unaambiwa, unaweza kukuta mtu ukamdharau kumbe ana madigrii ya sheria.

Loh! Hapo uoga ukamuingia Friday maana alijua akiongopa tu kaharibu, maana hao watu wanajua kila kitu, isipokuwa vya mapenzi ya kiafrika. Kwa hiyo asiyumbe.

Basi baada ya utambulisho huo uliochukua nusu saa, Madam Alexandrina akawaachia ubao Naima na Friday, yeye akaenda kujikalia zake chini kimya.

Naima akachukua marker na kuandika ubaoni.

MAANA YA UNYAGO, KUNGWI NA MWALI.

Yule mtafsiri akayasoma: “The meaning of Unyago, Kungwi and Mwali” wale wazungu pale kila mmoja akachukua kiitabu chake na kuandika kabisa siriaz.

Wakati huo Friday akawa ametumbua macho, akistaajabu Naima atazungumza kipi; maana yeye tayari uoga ulimuingia na kupoteza kabisa kujiamini. Lakini Naima akafungua mdomo wake na kusema yafuatayo:

Itaendelea..

KITUNGUU SAUMU 29

“Kwa kawaida wasichana wa Kiafrika hupata mafunzo ya kujitambua kijinsia na kujua majukumu yao katika jamii ndani ya darasa linaloitwa unyago, mara nyingi unyago huweza kuwa porini au ndani ya ua wa nyumba; mbali na wanaume,” alianza kusema Naima, mwenyewe akijishangaa midomo yake ikisema vizuri mno, na kwenye nukta akamuachia Jenny atafsiri kwa wazungu walioandikaandika na kutikisa vichwa vyao.

“Kwa wanaume pia wanaita Jando,” aliingilia Friday baada ya kuhisi atafunikwa bure.

“Ndani ya unyago, wasichana hufundishwa na walimu wanaoitwa kungwi, na hao wasichana huitwa mwali,” alisema Naima. Akimuachia Jenny atafsiri huku yeye akimeza mate kukumbuka maneno yafuatayo aliyoambiwa na Ilham.

Mara mwanaume fulani akanyanyua mkono. Aulize swali.

“Aar if women are mwali’s and you are kungwi! What about us men; And Mr Friday there?” (kwa hiyo, kama wanawake ni mwali, na wewe kungwi, vipi kuhusu sisi wanaume, na MR Friday pale)”

Loh! lilikuwa swali la kwanza, Naima akalipisha na kumtaka Friday ajibu maana ni la kiume, Friday akaanza kupagawa kidogo maana, sidhani kama kuna majina ya mwali na kungwi wa kiume. Doh sasa ajibu nini?

“technically, tungepaswa kuitwa kungwi na mwali pia, lakini wanaume hawependi kushea jina moja na akina mama hivyo hiyo hatuitwi jina lolote, pengine unaweza ukalazimisha kwa kusema, mwali wa kiume na kungwi wa kiume, lakini ni kitu ambacho hakipendezi, You Know!” alisema Friday, Jenny akatafsiri wale wazungu, Wakamgeukia Naima kuendelea na somo.

“Kwa ujumla, ndani ya unyago wasichana hufunzwa; miiko, uvumilivu na kubwa zaidi kujua tofauti yao na wavulana na hapo ndiyo safari ya mafunzo huanza. Sasa kwa kuwa nyinyi ni watu wazima na mmechanganyika jinsia, tumechagua masomo kadhaa na tutayafundisha kwa lugha nyepesi, lakini kabla hatujaenda mbali tutaanza na somo la kwanza ambalo ni hili: ” alisema Naima akielekea ubaoni wakati huo Jenny kama kawaida akatafsiri. Naima akaandika ubaoni maneno haya:

KUFAHAMU MWILI WAKO NA HISIA ZAKE.


KITUNGUU SAUMU 30

Kisha akasema: “UMESHAWAHI kuumwa halafu ukamwambia rafiki yako unavyojisikia?Je yeye alikwambiaje? Mara nyingi atakupa pole, lakini baada ya muda atasahau kuhusu kuumwa kwako na saa nyingine atakutaka ufanye kazi Fulani hadi umkumbushe kuwa haujisikii vizuri. Si ndiyo?”

Wote wakatikisa vichwa vyao kukubaliana na Naima.

“Ndivyo ilivyo hata kwenye suala la hisia za mapenzi. Asikwambie mtu wewe pekee ndiye unayetakiwa kujua hisia zako kwanza ndiyo uende hatua ya pili ya kuzijua hisia za mwenzi wako na baada ya hapo ndiyo msafiri pamoja kufurahia mapenzi yenu.

“Jinsi ya kujua hisia zako ni rahisi kwa mtu ambaye amewahi kujichua; ndiyo, ni tendo la aibu kusema wazi kuwa umewahi kujichua, lakini ni wazi kuwa wengi wetu tumewahi, na waliowahi wanazijua hisia zao vizuri mno yaani sehemu gani wakiguswa wanasisimka na kwa muda gani, tofauti na mtu asiyewahi.

“Sitaki ujichue ili kufahamu hisia za mwili wako, lakini naomba tukajichunguze kwa kujitomasatomasa wenyewe, tukatafute sehemu ya faragha kufanya hivyo,” Loh! tafsiri ilipomalizwa, makofi yalipigwa na wale wazungu wakisema hawajawahi kufunzwa mambo makubwa kama hayo na hiyo ndiyo kwanza ilikuwa siku ya kwanza tu. Naima akatabasamu na kushukuru, Friday akachanganyikiwa kidogo na kiwivu kikamuingia maana Naima alimstaajabisha na hakumpa hata kanafasi ka kuonekana

loh!

“Jamani, tunaweza kila mtu akaenda kutafuta faragha yake kuzijua vizuri hizo sehemu za mwili wake, kuna chumbani, kuna bafuni, kuna porini, tukutane hapa baada ya nusu saa!” alisema Madam Alexandrina.

Umati wote ukatokomea kila mtu alipopajua. Cha kushangaza hadi Madam Alexandrina mwenyewe, pale alibakia Naima na Friday tu, uzuri Naima baada ya kufunzwa na kungwi wa kiarabu mambo hayo, alijijaribu mwenyewe alipoenda kuoga bafuni asubuhi na akajiorodheshea sehemu zake. Hivyo hakuwa na wasiwasi, ila Friday alijitia kiburi na kusimama hapo, nafsi yake ikiungua kwa wivu.

“Friday, nimeongea vizuri!?” aliuliza Naima akishusha pumzi kwa furaha. Friday ndani ya chuki zake akajilazimisha kutabasamu na kujibu: “umefanya vizuri mno, umetisha!”




“Hayo yote ndiyo amekufundisha Ilham au?” alinyapianyapia Friday.

“ndiyo,” alijibu Naima.

“ooh nilijua umejitungia maana isije ikatuletea matatizo watu wenyewe kama unavyosikia wamesoma hawa wana madigrii hadi yanamwagika,ndiyo maana mimi mwenzako nimekuwa kimya!” alisema Friday akilenga kumkata confidensi mwenzake.

“We hapana, siwezi kutunga, mwenyewe nimetoka kufanya kila alichoniambia yeye, na mazoezi yote ya kiuno na mambo mengine nayafanya kisirisiri siachi,”

“ooh ni vizuri, sasa enhee wakishatoka huko kujichua, utawafundisha nini kinachofuatia?”

“oh hapo kuna vingi maana baada ya kujijua wao na hisia zao, watafuatia mazoezi ya kuzijua hisia za wapenzi wao pia, na wakishajuana ndiyo watapaswa kuheshimu hisia za kila mmoja kwenye mapenzi,; uzuri nimesikia wapo kila mtu na wake. halafu sasa baada ya hapo Kungwi aliniambia, tuwafundishe kipengele cha urembo na mapishi,” alisema Naima, Friday akayameza harakaharaka akipanga kumvizia Naima na kuyafundisha yeye yote. Lakini hizo mada za urembo na upishi zilimboa, akachukia maana zilikaa kikike-kike.

“Mh! Sasa Naima, huoni hili darasa utaliboa, wewe huoni kuna wanaume pia hapa, sasa hayo mapishi na urembo wapi na wapi?”

“Mh ila kweli lakini sina cha kuongea kingine lazima tu niwaambie kama kungwi alivyonielekeza, “ alisimamia msimamo wake Naima na dakika chache zilizofuatia, walioenda kujichua walirudi na walionekana wamejichua kweli maana wengine walirudi wakiwa wameoga kabisa.

“Naima, subiri mimi niendelee nao wewe utawafundisha mapishi,sijui na urembo,” alisema Friday akampiku Naima kibabe na kushika marker yeye akatabasamu mbele za watu akitafuta neno la kuanzia. Naima hakuwa na budi akaenda kukaa chini akimuachia Friday azungumze.

“Jamani nadhani sasa tumetoka kujichunguza na kila mtu atakuwa ameandika listi ya sehemu zake zenye hisia, si ndiyo?” aliuliza Friday, yule mdada wa kutafsiri akafanya kazi yake.

Wale wazungu wakaitikia: ndiyoo! Ya kiingereza lakini.

“okey sasa hapo nitataka mkusanye mniletee, lakini..” aliongea Friday lakini Naima akamkatisha na kumtaka amsogelee amwambie jambo kabla mtafsiri hajafasiri.

Friday akasogea kwa Naima na kuinama, amsikilize:


KITUNGUU SAUMU 32

“sikia, wasikusanye, waambie wapeane yaani wabadilishane hizo karatasi na wapenzi wao,” alisema Naima.

“Oh sorry, hizo listi mlizoandika naomba mbadilishane note book zenu na wapenzi wenu wazisome, kuna jambo la kujifunza hapo!” alisema Friday.

Wale wazungu wakabadilishana nadhani wasiokuwa na wapenzi hapo walikuwa ni wawili tu, mwanaume Fulani kijana handsome hivi na Madam Alexandrina mwenyewe.

So kwenye kubadilishana huko kukawa tatizo kwa hao wawili, Friday akaminyia jicho Madam Alexandrina na akachukua notebook yake. Kidogo yule kijana wa kizungu akatembea kumfuata Friday naye akampa na note book yake.

“Why are you giving me this?” aliuliza Friday akimaanisha kwanini unanipa mimi hiki?

“Oh I saw madam Alex giving you hers, so I thought you are helping us who have no partners, (nilimuona Madam Alex akikupa chake, nikajua unatusaidia sisi ambao hatuna mapatna), alisema kijana huyo ikabidi Friday achukue ile notebook yake pia.

Basi wakati umati ukiwa unasoma na minong’ono ikaanza chini kwa chini, Hata Friday pia akasoma ya Madam Alexandrina, akaona pale listi yake, akafunga note book yake na kumpatia.

Akataka kupotezea ile ya yule kijana, akanyanyua macho kumtazama akaona hamtazami, shauku ikamjaa kufungua; pale juu iliandikwa Collins, kwa hiyo Collins ndiyo jina lake.

Basi akaona ule ukurasa wa mwanzoni, sehemu za hisia zangu: vinido vyake, maana aliandika nipples, akashuka ya pili, matako, doh! Friday akashtuka kidogo mara akashuka ya chini, mamaaa! Nyuma, yaani kishududu ahja Loh! Mwanaume gani hisia zake zipo katika sehemu kama hizo kama siyo, gandu!? Basi Friday akarudisha ile notebook kwa Collins.

Alipompa, Collins alimtazama kwa jicho la mahaba mwalimu wake, Friday akatoka hapo amestaajabu kama nini.

“Okey jamani, tunachofuata hapa ni…” alianza kuongea Friday, lakini tena Naima akampa ishara akimtaka aende tena akamnong’oneze, aisee Friday akachukia kama nini, maana alihisi Naima anamchoresha kuonekana hajui chochote naye hakutaka aonekane hivyo mbele za hao wazungu.

“sikia Friday, hapo waulize kama walikuwa wakizijua hizo sehemu za wapenzi wao hapo kabla,” alisema Naima.

Itaendelea..

KITUNGUU SAUMU 33

Friday kabla hajasimama akaona hapo hata akiendelea ataharibu na kama kuitwaitwa na Naima ataitwa sana. Hivyo akaandaa kumkomoa. Akasimama na kusema: “Jamani samahani, mwalimu mwenzangu anajisikia kizunguzungu anaomba akapumzike kidogo, ni sawa?” alisema Friday bila kumtazama Naima, Naima akashtuka kuwa maneno hayo alimwambia Friday saa ngapi?

Basi Jenny alivyotafsiri tu, kila mtu alimpa pole Naima na tena Madam Alexandrina akamuita mfanyakazi fulani amchukue Naima hadi mapumzikoni, Naima naye hakuwa na budi zaidi ya kujifanya anaumwa kweli na kupelekwa chumbani kupumzika, njia nzima akijiuliza kwanini Friday alimfanya vile. Akakosa jibu!

Huko nyuma sasa Friday, akayaanza yale maneno ya Naima:

“aar.. sasa niwaulize swali? Je hizo listi za sehemu zenye hisia za wapenzi wenu, mlikuwa mnazijua zote hizo kabla?” aliuliza Friday na kuwataka waliokuwa wakizijua kabla wanyooshe mikono juu, waliokuwa hawazijui waache.

Aisee wakanyoosha nusu. Friday akajiongeza na kutengeneza swali la pili:

“Enhee, sasa nyie mliosema mlikuwa mnazijua; je mmeshawahi kuzifanyia kazi hizo sehemu za hisia za wapenzi wenu wakati wa kusex? ” aliuliza Friday.

Basi kati ya wale nusu waliojua wakagawanyika na wawili tu ndani yao wakanyoosha mikono juu.

“kwa hiyo hapo unaona ni wazi kuwa wengi wetu hatuheshimu hisia za wenzetu, na hilo ni jambo baya. Ili kuendelea na safari hii, lazima tutengeneze mrandano wa kimapenzi (chemistry) kati ya mwili wako na wa mwenzako, kati ya hisia zako na zake, lugha ya mwili iongee kati yenu.” Alisema Friday, wazungu wa watu wakaandikaandika.

Okey, hilo tulifanyie kazi. Lakini sasa nani yupo tayari kwa ajili ya mada kama: Kufanya mapenzi usiku mzima bila jogoo kuanguka; au jinsi ya kuwa na jogoo mnene mkubwa, au jinsi ya kuwa na kishududu cha motooo? Na kadhalika, na kadhalika!”

Doh aliposema hivyo kila mtu akashangilia na kuona ndiyo hayo sasa mambo.

“kwenye video za ngono, wanaume wakiafrika wana madudu makubwa yenye mistari ya mishipa mikubwa ya damu, Je wewe Mr Friday unayo?” aliuliza Collins kwa sauti.


KITUNGUU SAUMU 34

Friday akatabasamu na kuangalia sura za wanafunzi wake akaona wanasubiria kwa hamu kumsikia akijibu swali hilo.

“Of Coz, mine it’s Yam size. (ndiyo, yangu ni saizi ya gimbi)” alijibu Friday.

Watu wakapiga kelele wakisema kwa kiingereza: “Strip! Strip!” yaani: Vua! Vua!

Friday akamtazama Madam Alexandrina, Madam akatikisa kichwa chake kuonesha ishara ya kukubali.

Doh! Friday akavua nguo zake zote na kusimama, dudule likawa limening’inia chini, lakini urefu wake haukutisha, ona alikuwa na mwili mzuri wa mazoezi na misuli iliyojikata vyema. Kila mtu aliupenda hasa wanawake na wanaume walimtamani kama wangekuwa ndiyo yeye.

Lakini sasa dudule mbona la kawaida? Ikaanza minong’ono, lakini Friday alikuwa hajamaliza. Akasema:

“Mtu ajitolee anisimamishe,”

Jenny moyo wake ukimuenda mbio kwa jinsi Friday alivyomvuruga hapo, akatafsiri: “Any volunteer!?”

Basi wale wazungu kule wakagwaya maana walikuwa kila mtu na mpenzi wake kasoro hapo ni, Collins, Madam Alexandrina na Jenny mwenyewe ndiyo walikuwa singo.

Na Collins alionekana kuisubiria mno nafasi hiyo, akanyoosha mkono. Loh! Madam Alexandrina kama alijua vile kuwa Collins anamnyapianyapia Friday wake akasema: “Collins stop, Mr Friday is not a gay type; Let Jenny do it!” (Collins acha, Mr Friday siyo mtu wa mashoga, muache Jenny amfanyie)

Loh basi Jenny akitetemeka akaenda kumpapasa Friday, humu kwenye mapaja kuzunguka kwenye shina la muwa wa Bungala, sekunde tu kitu kikaanza kusimama kwa kasi , aisee Jenny akarudi nyuma akiogopa dudu aliloliamsha.

Watu wote walipoona wakasimama na kusogea karibu wengine wakilipima kwa rula, wengine wakilishika kuliona kwa macho, kupiga picha tu ndiyo kulikatazwa.

Naima akiwa ndani ya chumba chake, dirisha lililotazamia kule bustanini akaona kila kitu, saa hiyo ndiyo akajua kuwa Friday alimtoa kwa sababu ya wivu ili kuzoa watu, hasira zikamjaa, Naye vile mchaga ametumwa hela, huko Marekani hajaenda kuremba; akapanga lipizi lake.


ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

BLOG