Search This Blog

Monday, January 24, 2022

MCHEPUKO WA ZANZIBAR - 2

   

Chombezo : Mchepuko Wa Zanzibar

Sehemu Ya Pili (2)



Hata kazi zake hakuziwaza vizuri tena kila aalipofunga kope aliota vipochi vya manyoya, kila alipoalala aliota vitwangio na kinu.

Asubuhi alfajiri kama kawaida aliamka na kujiona mnara umesimama vilivyo tayari kunasa mawasiliano, akachukia na kuupindia kwa juu ya kaptula lake.

Akaingia chooni kuoga maji ya baridi ukavyonda walau. Akavaa nguo zake na kuondoka, koridoni akipishana na Sabrina binti Abdullah, aliyejitanda ushungi akidamka kufanya usafi.

“saa leko,” alisalimia Damian, macho yake makali yakipenya hadi ndani ya baibui ya Sabrina kuchambua dhima na maudhui anayoyatafuta kwa udi na uvumba.

“aleykum musalaam, shikamoo,” aliitikia Sabrina, mtoto laini. Babaye alimtega Damian kubadili dini amuoze, naye alikataa, sasa aliishia kula kwa macho tu huku misimamo yake ikitikiswa kila siku.

Naye hata hivyo alijiambia hatobadili dini na kuoa kisa nyege, hapana.

Hivyo basi Damian yampasa atafute kutimiza haja zake kwa njia ya wizi, wapi atafanya hivyo? Ilikuwa ni mtihani mkubwa mno.

Siku hiyo alifika dukani kwake, akasali sala zake na kufungua biashara zake kama kawaida. Akapata wateja wake wa asubuhi na mchana, baadaye akaja Bushiri kupiga soga huyu alikuwa na marikiti ndogo pembeni. Nao waliweka kibenchi pale nje.

Bushiri huyu alikuwa rika sawa na Damian, yeye alipata kutembelea Dar kidogo hivyo hakuwa mwenye mada moja walizungumza mengi tu,hata kuhusu wanawake wa Zanzibar.

“Bwana Damian, unajua unawahi sana kufunga duka, funga walau saa nne,” alisema Bushiri.

“hapana, saa nne usiku sana na giza la huku nitashindwa kurudi nyumbani aisee,”

“sikiliza, unakosa mambo, unajua wavuvi saa kumi na mbili wanaenda kuvua, wanarudi alfajiri, huku nyuma kijiji chote wanabaki wanawake tu, wanawake ndiyo usiku kuanzia saa moja wanatoka kutafuta mahitaji yao muhimu, sasa maduka yote wanakuta yamefungwa, ila ukifungua wewe, utawaona wanawake wanakuja kununua, au huwataki!?” alisema Bushiri, ikawa ni wazo zuri maana kusema za ukweli tangu Damian afungue duka hakuwahi kumuona mteja wa kike akifika hapo hata kwa Bushiri pia, alitaka waje walau apate tahfifu loh.




Wakakaa kweli wakipiga soga na kufanya biashara hadi saa moja, kuanzia hapo sasa Jambiani kukapoa, kukawa kimya na kiza totoro, ni wao tu ndio waliiokuwa na mwangaza wa kandili pale dukani mwao, kwenye vijumba vingine kulikuwa na vibatari tu vikionekana kupitia madirishani.

Hapo wakasikia hata bahari iliyokuwa magharibi mwao ikifoka kwa kutema mawimbi pwani. Kundi la mwisho la wanaume waliowaona lilipita wakiwa wamebeba nyavu, pondo na injini na nanga wakiingia baharini.

“Sasa wanaume wote wamekwishaondoka, na taa zetu zinaonekana kote kule kwenye majumba, utaona tu purukushani za wanawake zinaanza,” alisema Bushiri.

“kwanini purukushani zianze wakati wanaume wameondoka!?” aliuliza Damian.

“sikia, nikupe udhaifu wa wanaume wa visiwani, huku bwana wanaume hawana muda na wanawake wao, wengi hukesha baharini, usiku kucha, hurudi asubuhi ya saa moja, hapo hufikia ferry kufanya mnada wa samaki, wakishauza, hurudi nyumbani saa nne au saa tano, wakifika walala hadi saa kumi jioni, wakiamka hapo ndiyo wanapumzika hadi saa kumi na moja waanze kusuka nyavu zao na kuandaa mashua, saa kumi na mbili ndiyo wanaondoka baharini kama unavyoona, sasa hapo niambie wanafanya tendo saa ngapi? Na baharini hutakiwi kwenda na janaba maana ni mkosi chombo chaweza zama,” alisema Bushiri na kuongeza: “Sasa hapo kusema za ukweli, wanawake wao wamejaa ashki, usiku wanahangaika, utawaona tu, wanavua majuba na mabaibui kujichekesha tu;

Basi wakakaa Zaidi, Damian saa akaona haziendi, akatazama mwezi na kuuona ukiwa sehemu Fulani ya zenith, akagundua ni saa mbili hiyo, na mpaka hapo hakukuwa na mteja yoyote aliyefika dukani mwao.

“oya, tukalale bwana,” alisema Damian.

“Usikate tamaa, siku ya kwanza inakuwaga ngumu kama hivi, kwa sababu hawajazoea kuona duka likiwa hadi sasa hivi, we subiri tu, hebu ona huyo nani anakuja!” alisema Bushiri akimuonesha kwa ishara Damian.

Kwenye giza akatokea mwanamke, na msichana, walitembea kwa adabu lakini cha ajabu hawakuwa na ushungi wala kujitanda mwilini, wakasogea kwa tahadhari na kuuliza kwa sauti.




“eti hapo mwauza duka! Na marikiti!?”

Ilikuwa ni sauti mwanana yenye lafudhi ya Kiswahili cha visiwani haswa. Bushiri akasema kwa sauti; “ndiyo twauza hadi usiku siye!” Waliposema hivyo, vicheko vya kike vikawatoka hao wakina dada, wakati wakijongea Zaidi kwenye mwangaza wa walipo akina Damian na Bushiri.

Damian kwa mara ya kwanza akaona wanawake wazuri, rangi, ngozi, nywele macho yao, vipua vyao, vimidomo, na la vifua vyao vikamtia ganzi, hapo hakuona hata kasoro zao za hao wasichana hao kutembea peku na kukosa matako makubwa kama wanawake wa Kiarusha. Yeye aliona johari tu kwenye roho yake.

“kaka wa duka, mie ataka kiberiti, ataka leso ya kike na sabuni,” alisema huyo msichana mzuri Zaidi mdogomdogo, mwingine akiwa amesimama nyuma yake akitazama huko na huku.

“kiberiti, senti moja, Leso senti tatu na sabuni senti mbili, jumla senti sita,” alisema Damian akichangamka kinoma. Huku chini tayari akiwa ameshawaka gari lake na suluari ikimloa na kujikojolea angali akizungumza tu na hao wasichana.

“hiyo hapa, halafu Bushiri huyu mbona azungumza vibaya, anichekesha mie,” alisema mwingine akicheka kabisa kwa vile Damian anavyozungumza kichaga.

“haha, huyo mtu wa bara, wa kule kwenye mlima Kilimanjaro kama wapasikia, aitwa Damian,”

“Damwani,” alisema mwingine akijaribu kuliita jina la Damian.

“hapana Damian,” alisema Damian mwenyewe.

“mh aya, asanteni, sie twaenda, tutakuwa twaja usiku kumbe duka mwafungua, basi mtatupa nafuu,” alisema mwingine.

“wadada, mmejua jina langu na mimi niwajue basi,” alisema Damian.

“mimi Habiba, huyu dada angu Shahida,” walisema na kuondoka wakichekacheka, wakatembea kama wanataka kubakia lakini kama wanataka kuondoka pia. Ni wazi kuwa walikuwa na ashki kama alivyosema Bushiri na Damian aliligundua hilo kwa sababu na yeye mwenyewe alikuwa katika hali hiyo pia.

“Damian, umeonaaa!?” alisema Bushiri kwa furaha.

“Loh nimeona kaka, nitakesha kila siku, yesu na maria,” alisema Damian. Akakaa kimya akiona msichana mwingine akitokea kwa mbali.



“habari zenu, nimetumwa kiberiti na mafuta ya kuwashia,” alisema binti mzuri mno kuliko wale wa mwanzoni, Damian suruali ikamchafuka tena akahema kwa kufikia shindo lake.

“haaaaah! Karibu,” alisema Damian akiganda kwanza kumtazama vizuri binti huyo kama ni jini au mtu haswa.

“naomba nipatie basi, mie niende na zangu,” alisema tena huyo msichana aliyeonekana kuwa na haraka mno kuliko wale wa mwanzoni.

Haraka Damian akampatia kiberiti na mafuta kumtilia kwenye kichupa chake, kisha akampa na kumshika walau mkono wake kijanja.

“samahani msichana unaitwa nani?”

“naitwa mama Aymar,” alisema.

“umeolewa?” alisema Damian kwa mshangao.

“ndio kwani wewe hujaoa?”

“hapana sijaoa,”

“mwanaume mzima umejawa ndevu hujaoa! wasubiri nini?” alisema huyo Mama Aymar akianza kutembea.

“sikia mama Aymar, mimi naitwa Mangi, na wewe nitajie basi hata jina lako,”

“Naitwa Naifathy,” alisema hivyo huku akiyoyoma.

“kaka, usijaribu kumtongoza yule, utakufa, mumewe ni Mzee Salum bin Salum.”

“mumewe ni mzee?”

“ndiyo ana wake wanne, huyu ndiyo mke wa mwisho,”

“mzee mwenyewe yupo wapi?”

“ni mtu wa baharini, alipita hapa mchana, ana busha hivi kubwa,” alisema Bushiri.

“duh, sasa anamudu vipi wanawake wanne, wakati mvuvi halafu ana busha!”

“hiyo ndiyo miujiza ya Mungu hapo sasa. We tongoza wake za watu wowote huku lakini nakuomba kwa usalama wako usimtongoze huyu wala wake wengine wa yule mzee, wakipita hapa nitakuonesha.”

“agh! kwani hamna wasio wake za watu huku?” aliuliza Damian.

“Huku utampata wapi binti asiye mke wa mtu? Sikia, wakiwa tu na miaka kumi na nne, mabinti hutafutiwa waume kabisa, ndiyo wanasubiri akue aolewe, hivyo huwezi kupata mwanamke labda ubake watoto , hivyo bora wake za watu, japo nao kurogwa nje nje,”

“wee mimi siogopi nimeaga kwetu, nimechanjwa na chale, mimi nilishampenda huyu Naifathy,” alisema Damian.

“mh, sawa, mimi nataka niwapitie wote wale wawili wa mwanzoni,” alisema Bushiri akionekana mroho mno Japo yeye tofauti na Damian, alikuwa ameoa na mkewe alikuwa huko Unguja mjini.



Basi baada ya hapo dukani na gengeni wakawa wanafika mabibi na wanawake wengine wasioridhisha kwa sura zao, wengine Damian alistaajabu kwani walikuwa weusi tii lakini sura zao kama waarabu kabisa, Hao hakuwapenda hata kidogo.

Moyo wake ukawaka kwa Naifathy, mke wa nne wa mzee Salum bin Salum. Akaapa atalala naye hakika.

Hadi saa nne wakati yeye na Bushiri wakifunga biashara zao na kusindikizana kurudi njia kuu, tayari walikuwa wamefanya biashara kubwa mno tofauti na waliyoifanya mchana.

“kesho tutakaa tena hadi usiku,” alisema Damian akionekana kunogewa tayari.

“haina shaka haha, usije ukamaliza hela zako kwa kuhonga,”

“weee mimi mchaga, hela kwanza, mapenzi baadaye, sijaja kucheza huku,” alisema Damian.

Akarudi kwa njia yake hadi nyumbani alipopanga, akagonga mlango na kufunguliwa na Sabrina katoto ka mzee Abdulrahman, akakaona kakiwa hakajitanda, akakashukuru na kuingia ndani zake, taswira za Naifathy zikamkosesha usingizi. Japo alijichafua mara mbili nzima pale dukani, lakini dudule hamu haikuisha lilisimama tena.

Akachukua mafuta, na kupakaa, akalichuachua huku akivuta taswira kabisa kama vile anamuingiza kunako Naifathy, na ile sauti yake ikimlilia sikioni kama kweli vile, akachukua muda taswira zake zikimlaghai akajiona tendoni kweli; basi hitimisho tamu hatari likamfika, dudule likatoa udelele. Utimamu ukamrudia kuwa kumbe alikuwa akivuta tu picha na wala Naifathy hakuwa pale na yeye.

Akakereka na kujifuta, kisha akalala, akijiapiza lazima kujichua kukome, lazima ampate Naifathy.

Asubuhi kama kawaida, akaenda kufungua kiduka chake, akijiona mpya kidogo, akakutana na chizi mwenziye Bushiri aliyekuwa akipanga nyanya, vitunguu maji na binzari.

Pamoja wakaanza kuuchora mtaa.

“ona sasa umemuona yule mzee aliyeshika samaki, yule sasa ndiye mzee Salum bin Salum,” alisema Bushiri akimuoneshea mzee Fulani mweusi, mwenye manywele yenye mvi, kuanzia kichwani hadi mikononi, ambaye kavaa msuli mkuukuu na anatembea kwa tabu kidogo.

“yule ndiyo mumewe Naifathy?”


ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

BLOG