Search This Blog

Monday, January 24, 2022

KITUNGUU SAUMU - 5

   

Chombezo : Kitunguu Saumu

Sehemu Ya Tano (5)


“kwani wewe Madam kakwambiaje?” aliuliza Friday akiyeyusha swali la Naima.

“ameaniambia niendelee kupiga kazi, amenisanisha mkataba wake uleule na amesema ananipenda ninavyofanya kazi kwa sababu watu wananipenda pia,” alisema Naima, maneno hayo yakamuingia Friday rohoni. Akagundua kuwa muda wote alikuwa akipigana vita kimakosa, sasa abadili mbinu na mbinu ya kumng’oa Naima ni kumfitinisha na wanafunzi wake maana wasipomkubali wao uhakika kabisa ndiyo Madam atamfukuzia mbali.

Itaendelea..


KITUNGUU SAUMU 45

“sasa Friday tuache upuuzi twende tukafanye kazi, bwana,” alisema Naima.

“okey, kwa hiyo utakuwa unaniongezea laki tano kweli?,” aliuliza Friday.

“hiyo ni shukrani yangu kwa kunipa hili dili,”

“aya asante,” aliitikia Friday kwa sura ya nje akionesha amemaliza bifu lakini ndani kwa ndani alikuwa bado na lake.

“poa twende basi darasani, wanafunzi tayari wameshajaa, vipi unakumbuka aliyotufundisha kungwi jana?” aliuliza Naima.

“ndiyo,”

“haya twende tufundishe tuwafanye watupende, wakitupenda hawa mbona mishahara itaongezwa tu,” alisema Naima akimtia moyo Friday.

Wakatoka hapo wakiongozana hadi kule kwenye bustani, wakaanza kwa kuwasalimia wanafunzi, wakawakaribisha wanafunzi wapya pia na kukumbushia kwa kifupi waliyojifunza jana yake.

Kisha Naima akachukukua marker na kuandika ubaoni kichwa kirefu cha habari.

“JINSI YA KUWA MWANAUME NA JINSI YA KUWA MWANAMKE AFRIKA,”

Kama kawaida Jenny akatafsiri yake, wote wakawa kimya kuandikaandika walichoambiwa.

Ndio sasa Naima akaanza: “mapenzi ni mchezo unaoanzia mbali sana kabla ya kufikia kuangushana kitandani. Hata nyinyi mna desturi zenu. Lakini kwetu japokuwa tunazaliwa wanaume au wanawake, bado kuna jinsi ya kuwa mwanaume na jinsi ya kuwa mwanamke na yote hayo tunafundishwa unyagoni kwa tuliobahatika na wengine hufunzwa na wazazi wao,” alisema Naima, akamtazama Friday wakati Jenny akitafsiri.

Friday akasimama na kusema: “Kwetu sisi wanaume kiasili tunafundishwa jinsi ya kuwa viongozi, tunafundishwa jinsi ya kuzungumza kwa sauti ya mamlaka, tunafundishwa ujasiri wa kufanya kazi na kuleta mahitaji nyumbani, kusimamia familia, tunafundishwa kuchukua hatua kwenye matatizo na zaidi tunafundishwa jinsi ya kumtongoza mwanamke, kufanya naye mapenzi, kikubwa zaidi, kulinda selebobo letu na kutoruhusu mwanaume mwenzako akufanyie dhihaka au dharau, kwa sababu hiyo inatushusha uanaume wetu,” alisema Friday kwa mara ya kwanza naye akipangilia maneno yake, vile viingerezangereza alivyokuwa akivichomeka siku za nyuma hakuviweka siku hiyo.

Naye akamtazama Naima, aliyesimama pembeni ya ubao, nakapokea na kuanza kuzungumza pia, akasema:

KITUNGUU SAUMU 46

“Kwa sisi wanawake, tunafundishwa cha kwanza, jinsi ya kuwa wasafi wa kila kitu kinachotuzunguka, warembo, wachapakazi hasa kupika,kufua, kumtunza mume na watoto na kubwa zaidi kumtuliza mwanaume kwa mapenzi hapo ndiyo kuna mambo mengi kama: kujiweka kikikekike yaani kilainilaini hivi; jicho lirembue, midomo ibetue, kiuno kibinue, shingo iinue, sauti isisimue, mwendo uvutie; bila vitu hivyo, wanaume hawatakupenda,” alisema Naima, akimuachia mtafsiri kisha Friday akapokea tena maelezo na kuongea: “Kwa hiyo basi leo tutajaribu kwa vitendo kwanza na baadhi ya wanaume hapa halafu tutahamia kwa wanawake na kungwi Naima,” alisema Friday mwenyewe akifurahia jinsi alivyoweza kutiririka kwa step, hata Madam Alexandrina aliyekuwa ameketi chini akatikisa kichwa akiona darasa linavyonoga kwa jinsi Friday alivyojipanga vizuri siku hiyo.

“Mr Beacons, nataka utembee kuanzia huko kiumeume hadi hapa, halafu sema: siwapendi wajinga!” alisema Friday.

Akasimama huyo mtu mzima, akatembea tu kawaida hadi alipokuwa Friday kisha akasema kikawaida: I hate fools. Darasa zima likiangalia huo mfano. Mr Beacon akarudi kuketi. Friday akaenda yeye kukaa kisha akasimama na kuanza kutembea sasa.

Akakanyaga ardhi ikalia tiih! Tiih! Akatembea kwa mikogo dume taratibu lakini kikakamavu. Uso ukiwa siriaz. Mikono akiirusha kwa stadi kama hewa yote ya kwake. Halafu akageuka na kusema kwa hasira na hisia:“I hate Fools!”

Doh wazungu wa watu wakapiga makofi kuonesha kuwa somo limewakolea, mtu mmoja tu hakuwa na furaha hata kidogo hapo naye ni Collins, nadhani alisubiri somo la kike maana nani kasema yeye mwanaume!

Kutaka sifa; Friday akaiweka ile sauti yake ya bezi, azungumze kama anazungumza sasa kwa furaha na rafiki kisha akamgeukia Naima na kuongea kama anaongea na mpenzi wake; kote huko sauti ilikuwa tamu nzito na ya kiume.

Sauti ni silaha, sauti nzito ni uanaume, wanawake hawapendi mwanaume akibana sauti maana na hata mkizibana vipi hamuwezi kuwazidi wao kwa unyororo wa sauti zao; kazeni sauti zenu bwana!” alisema kwa sauti Friday, yakapigwa makofi tena zaidi.

*Eti wanaume wanaobana sauti wakizungumza wapoo?! Itaendelea..


KITUNGUU SAUMU 47

Wakaenda mapumziko kisha wakarudi Naima akichukua usukani, akawafundisha waali wake jinsi ya kutembea kwa kujishongodoa, kujishaua, kukaa kihasarahasara, kubonga kwa sauti ya puani, nakadhalika na kwa Naima ikawa pongezi hadi fujo.

Wakaingia kwenye mapenzipenzni na kuwafundisha wazungu wa watu, masaji za mkia wa kondoo, na faida zake kama kubana hivyo vishududu vilivyolegea kwa uzazi, kumkuza balanguru kwa akina baba, na kuongeza dakika za kupiga shoo. Doh sararee, wakamtaka Naima asaule waoneshwe wazi.

Naima akavua na kubakia na kichupi tu akalala juu ya kitanda cha masaji kilicholetwa hapo, Ikawa Friday akampakaza na kumchua Naima, huku akielezea zaidi na zaidi, lakini umbo la Naima japo lilikuwa la kuvutia lakini kila mtu aligundua michirizi mibaya ya tumbo, lakini hakuna aliyethubutu kuyaongea.

Ikafika wakati kichupi kikatakiwa kuondolewa, ili kupakwa huko kunako, Doh ilikuwa shida kwa Naima lakini alizuia hisia zake na kupakwa kote, kisha na yeye akamfanyia hivyohivyo Friday na kumsugua yale mafuta kwenye rungu lake hivyohivyo huku akielekeza.

Aisee wanafunzi walidata. Vikaletwa vimasajio kibao pale nje, wakaanza kupakazana chini ya maelekezo maalumu.

Asikwambie mtu, siku hiyo somo la upishi lilisubiri maana hawakuishia hapo wale wazungu, wakakoboana kabisa maana mipako ile iliwashinda na mafuta yale jinsi yalivyoteleza na umotoumoto wake ulivyowahamasisha ilikuwa balaa.

Naima akazuia hisia zake na kukimbilia chumbani, akaoga na kujisafisha siri zake maana hakuweka vidonge vile asubuhi kwa ajili ya lile somo, sasa akaenda kuoga na kuviingiza tunduni vile vidonge vya mwisho kama unakumbuka alikuwa na tatizo la fangasi.

Basi akiwa humo chumbani akaanza kuendelea na mazoezi yake, ambayo tangu siku ya kwanza alikuwa akiyahangaikia kama nini, ya kukata kiuno. Akajinyonga akijitahidi tumbo lisihusike, miguu isimcheze, kiuno tu kinyongeke, lakini kila mara akashindwa kukipatia zaidi. lakini angalau saa hiyo kuliko zamani alikuwa hajui kabisa.

Siku hiyo hela zilizongia kwenye akaunti yake, zilimchanganya akajifua kwa bidii mno hadi kieleweke maana hofu yake ilikuwa itakuwaje kama atafikia somo hilo la kiuno halafu akashindwa kutoa mfano?


KITUNGUU SAUMU 48

***

“Friday, please I love U, just fu*k me once,” (Friday nakupenda naomba unifanye mara moja tu) alilia Collins akiwa ameingia chumbani kwa Friday.

“hapana Collins mimi nawapenda wanawake, sikukatai kwa ubaya lakini,” alijibu Friday.

“Sawa, basi naomba tu nifanyie hiyo masaji niisikie maana mimi nimekosa patna,” aliomba Collins akizidi kumtega Friday. Friday akawa kama amekumbuka kitu hivi.

“Hapana Collins mpaka unifanyie kitu kimoja hivi, nitakufanyia masaji hadi utapenda,” alisema Friday.

“niambie kipi?” aliuliza kwa shauku Collins

“Nataka kwanza ukamrekodi Adellah chumbani kwake akifanya mazoezi,” basi hakumaliza kuongea Friday, Collins huyo akapepea kwenda kutafuta kwa kumrekodia Naima, akapita njia za juu za dari, akavizia kwenye tundu la hewa, akichungulia chini akimuona Naima akihangaika kujinyonga, akatega simu na kumrekodi.

Akarudi haraka mno Friday akishangaa kuona shoga karudi haraka hivyo. Collins akamkabidhi Friday ile video na kujilaza kitandani akimtaka Friday amkande sasa.

Ahadi ni deni Friday akalazimika kumfanyia masaji ya mafuta ya mkia wa kondoo Collins, maana aliona akimtumia shoga huyo vizuri mambo yatakuwa poa katika kumshusha Naima. Basi akalikanda hilo gandu la kizungu hapo, likigugumia tu utamu na kumtaka Friday aligandue kabisa.

“sikia, kesho nataka darasani unyooshe mkono umtake Adellah awaoneshe jinsi ya kukatika, nataka umkomalie kidogo, halafu akishindwa mpelekee hiyo video madam Alexandrina aione, kuwa kungwi wake hajui viuno, ukitoka hapo njoo nitakukuna utakavyo!” alisema Friday, Collins akatabasamu na kuondoka zake akiwa amepania panupanu kuifanya kazi aliyoambiwa na Friday.

Friday huko nyuma akacheka tu maana alijua akimpiga safari hii Naima hatoki kwa kuwa anampiga kwa kutumia wanafunzi wake.

Wakati anawaza hayo Friday, mara akapigiwa simu akiitwa na Madam Alexandrina chumbani kwake.

“Friday, umenifurahisha sana leo; lakini kingine nataka na mimi unifanyie masaji hapa ndani na labda tutazungumzia mshahara wako vizuri,” alisema Madam Alexandrina akijimwayamwaya na kibikini.

Friday akaona hapohapo ndiyo kwa kumsugua huyo Madam hadi aongeze mshahara umzidi Naima, mfyuuuu.

Itaendelea..

KITUNGUU SAUMU 49

Basi Friday akamlaza Madam wa watu na kumchuruzisisha mafuta taratibu akimwagizia kuanzia mgongoni na kushuka ikweta. Akaanza kulipaka gongo la madam kwa ustadi, mbongo yule, akalikoleza kandole. Akaongeza mikando usawa wa kiuno akapanda kwenye eneo ambalo kitaalamu laitwa ‘Lumbar Vertebra’ hapo ndiyo kwenye mzizi wa nyonga.

Akamlowesha kwenye wowowo, na kulichua la kushoto kisha la kulia, akitafuta msuli mkuu wa tako, uitwao, Principal Maximus, akatumia dakika moja na kumpambanua katikati, akapekenyua mfereji wa Suez, na kuchua sehemu vyanzo ya marinda doh! Madam hakuwahi kufanyiwa hivyo, akalia kwa sauti kuu: “aaa eee iiii ooo uuu.”

Mshenzi Friday kama kichuya uwanjani, akajitia futa na yeye kifuani pake, kisha akamlalia Madam na kuanza kumtambalia juu kama nyoka, kitu ngozi kwa ngozi. Akagundua Madam alitamka irabu moja tuu wakati mafuta yakimuingia kunako; “ooooo, ooo!”

Madam yakamshinda, mautundu ya kibongo, akajibinua, sime la Friday limuingie maana lilimpangusapangusa eneo la Misungwi; likapenya mwanzoni, lakini Friday mjanja aliyesoma alama za nyakati alipohisi Madam anakolea, akalichomoa na kukaa kitandani, akishika tama.


“aaaaah nini Friday nitakuua! Nitakuuua!?” alilia Madam Alexandrina akigalagala kitandani muonjo ukimuwasha.

“Madam sina mood, leo!” alisema Friday.

“sikia nakuongeza milioni tatu na nusu kuzidi Naima njoo,” alilia Madam.

“nitaaminije?”

Madam kama chizi akainuka na kuandika cheque harakaharaka, ya milioni sita. Nje ya mshahara,akasema hiyo ni dhamana.

Friday akafurahi na kuingia kulisasambua tena, alipomaliza akatia kofi kwa kumuhangaisha Madam.

***

Wakati huo huko ndani Naima alikomaa akakomaa hadi kiuno kikamuuma, akachoka na kulala.

Usiku aliamshwa na Friday wakaenda kula na kurudi kumsikiliza kungwi aliyewafundisha mada ya kesho yake.

“aaah Naima bado kiuono ee!?” aliuliza Ilham.

“ndiyo, nakaribia kujua kungwi, najitahidi,” alisema Naima kwa upole.

“basi usijali, endelea na mazoezi utajua tu, wiki haiiishi, tutaendelea na mada nyingine, au siyo Friday?” alisema Ilham, Friday akaitikia moyoni mwake akijua fika kuwa kesho atakinukisha.


KITUNGUU SAUMU 50

Basi bwana kesho yake ikafika.

Darasa likafurika kama nini maana ilisikika kuwa kuna kundi jingine limehama kutoka chuo Fulani hivi kinachofundisha elimu ya mapenzi na kuhamia hapo. Chuo gani sikijui, lakini wote walisikia kuhusu elimu ya mapenzi ya kiafrika inafundishwa kwenye chimbo Fulani, na waafrika wawili hatari, ndiyo wakaja hapo kujiunga.

Kama kawaida Naima na Friday wakawasalimia wanafunzi wao na kukumbushia ya jana, wakaona akina baba wakikaza sauti na kutembea kiume na akina mama na Collins wakitembea kwa mapozi na kujishongondoa.

Hahaa! Ilichekesha lakini ilipendeza na hata hao wanafunzi wapya wakashangaa na kuwaonea wivu wenzao.

Siku hiyo basi wakaanza na somo la sauti za mahaba. Na umuhimu wake. Zikazungumziwa huko na kwa vitendo kabisa. Kila mtu akitoa sauti zake za mahaba yake, doh wengine walikuwa wanasauti za ajabu, wengine hawana, hahaa! Darasa lilichangamka hatari.

Sasa palepale Collins akanyanyua mkono kama Friday alivyomwambia jana.

“kungwi Waafrika wanasifika kwa kukata viuno kwa staili mbalimbali je, unaweza kutuonesha japo na sisi tuanze kujifunza, Kabla hatujafikia somo hilo?” aliuliza Collins wakina mama wakapiga makofi mno.

“yah ni vizuri, na nitaandaa hivi karibuni, tutaanza kujifunza pamoja,” alijibu Naima. Collins akafanya “buuuuuuu!” kama anazomea vile. Doh! akajishtukia maana wote walimtazama yeye akiwa amekosa sapoti maana alifanya vile ili zomeazomea zianze.

Kuvunja hiyo mada, ikawa Naima akaleta mbele dawa Fulani hivi akikabidhi kwa ajili ya uchunguzi kwa yule mkemia, Madam Magreth akiisema dawa hiyo ni ya kumkausha maji Hadija-Milenda, kumtoa fangasi,harufu mbaya na kumfanya awe amebana, kumuongezea joto hata kama kapitisha watoto kumi na ina matokeo ndani ya siku moja tu.

Aisee aliposema hivyo wanawake wakaanza kupapatikia wakitaka uchunguzi ufanyike haraka sana maana wakina mama wa kizungu walikuwa na tatizo hilo hatari.

Somo liliisha, Collins akimbania jicho Friday na kumfuata Madam Alexandrina ofisini mwake. Nadhani huko sasa alienda kumuonesha video ya Naima akishindwa kukata kiuno.

“Uwiiiiii!”

Itaendelea..


KITUNGUU SAUMU 51

Basi Collins akafika mlangoni kwa Madam Alexandrina kwa mbwembwe zote akagonga mlango, moyoni akiliwazia dungu la Friday.

“Collins nikusaidie nini?”

“Kama mwanafunzi ninayelipia ada kujifunza hapa, nimegundua jambo linalonifanya niwe na wasiwasi na mwalimu wangu kama anachotufundisha ni sahihi au ni uongo,”

“Una maanisha huna uhakika na mnachofundishwa?

“Ndiyo maana biashara siku hizi zipo kila sehemu hata kwenye dini, so, kwanini niwe na uhakika sana na nyinyi?!!” alisema Collins akijinyorodoanyorodoa kishogashoga akihakikisha maneno yake yamemuingia kunako Madam.

“Sikia Collins embu nielezee vizuri!!”

“Madam, nina wasiwasi Adellah hajui mambo anayoyafundisha,”

“aagh Adellah ni mtaalamu anajua na wewe ni mwanafunzi mmoja tu unamlalamikia, labda kwa sababu ya wivu na inda zako binafsi. Muacheni Adellah wangu!” alitetea Madam Alexandrina.

“oh kumbe ipo hivyo? Basi ngoja nikasambaze hii video kwa wanafunzi ili wamjue Adellah vizuri na labda kesho asubuhi wote tutaondoka na kurejea kwenye darasa la Mr &Mrs X,” alisema Collins, Madam akashtuka na kumtaka Collins amuoneshe hiyo video ni ipi.

Collins akamkabidhi simu yake Madam ajionee ile video yaNaima akijifunza kukatika. Looh! Madam macho yakamtoka pima. Jazba ikapanda akatoka kwa hasira hadi kwa Naima. Akaingia ndani bila hodi.

“ What the fuck is this Adellah?!” hiki nini Adellah!” alifoka Madam. Yaani kwa hasira zile hakukuwa na haja hata ya Naima kumuita Jenny amtafsirie kwa kuwa maana ilionekana wazi tu.

Naima akaitazama video yake aliyooneshwa na Madam, Loh! Akaishiwa nguvu.

Sasa Friday akiwa nje tu ya mlango akamuona Jenny akitembea koridoni, akamwambia Collins amuongeleshe na kumtoa asiingie kwa Naima. Yeye kwa kuwa aliisubiria mno nafasi hiyo akaingia humo chumbani kwa Naima akijifanya anaulizia kinachoendelea.

“Umeona hii video Friday? Hivi ndiyo mnavyotarajia kuwafunda wanafunzi wangu? Hivi mnadhani kuna vikundi vya mafunzo kama hivi vingapi kwenye jimbo hili pekee? Mnadhani niliwezaje kuwashinda wote ndani ya siku chache tu na kuwa zaidi yao?

KITUNGUU SAUMU 52

”Ni kwasababu nimeamua kuelemea kwenye asili, nikiwa na wafundishaji wa kitamaduni, na hapo namaanisha wewe na Adellah hapa, lakini nilikuwa nimekosea, ningekusikiliza awali ulivyoniambia nimlete Adellah original hapa na siyo huyu mamluki!” alisema Madam Alexandrina.

Naima japo hakuelewa lakini aliposikia neno real Adellah na kusontewa kidole kwa chuki, akahisi lazima kibarua kitakuwa kimeota nyasi. Loh! Akapiga magoti akilia na kumuomba Friday amtafsirie Madam majuto yake.

“Friday, mwambie Madam, ndiyo kuna baadhi ya vitu sivijui lakini ninafundishwa na mtu mkubwa sana na nitajua tu haraka sana, mwambie Madam, asinifukuze tafadhali; nipo tayari kufundisha kwa robo mshahara, tafadhali mwambie Madam nimekosa lakini makosa yangu nitayasahihisha, anipe siku mbili tu nitajua kukatika,” alilia Naima.

Friday alivyokuwa nyoko akayageuza yale maneno na kumtafsiria madam maneno yafuatayo: “ Naima anasema kweli hajui chochote na hata aliyokuwa akiyafundisha aliyaiba kutoka kwa Adellah, anaomba msamaha kwa kukudanganya, anaomba umpe siku mbili tu aweze kuandaa vitu vyake arudi Tanzania maana darasa lako linazidi kumshinda kila siku, alikuwa anaogopa tu kukwambia mwanzoni, anasema bora umlete tu Adellah,”

Madam aliposikia hivyo akaondoka kwa hasira zaidi maana alimpenda mno Naima na sasa kumbe yeye ndiyo anataka kuondoka, shit!, Baada ya fitina zake Friday akatabasamu kwa jicho la kijani, akaingia ndani kwake na kumpigia simu Adellah Tanzania.

“sikia, nimeshamharibia Naima kwa Madam, lazima tu arudishwe na wewe uje? Ukija nataka unipe mambo kama ulivyoniahidi, sasa kama unaweza mpigie simu Madam sasa hivi.”

Basi Adellah akampigia simu Madam bila kuchelewesha.

“Hallow, Adellah, I was about to call you this instant, listen, I want you here no matter the cost!” (adellah nilikuwa nataka kukupigia sasa hivi, sikia nakutaka huku kwa gharama yoyote ile)” alisema Madam Alexandrina.

“I’m ready even now!” nipo tayari hata sasa”. Aliongea kwa furaha Adellah.

“Okey some one will contact you soon!” sawa mtu atakupigia sasa hivi!” alisema Madam Alexandrina akizungukazunguka ofisini kwake.

Itaendelea..


KITUNGUU SAUMU 53

“Mbona unalia?” aliuliza Jenny baada ya kumuona Adellah akijiliza hali amelala kitandani.

“we acha tu,”alisema Naima akilia zaidi.

“niambie nini tatizo?”

“nimeharibu kazi Jenny, nahisi nitafukuzwa!”

“kwani umefanya nini?” aliuliza kwa shauku Jenny, doh ikabidi Naima azungumze ukweli akimhadithia Jenny tangu mwanzo hadi alipofikia kushtukiwa na Madam Alexander kwa ushahidi wa video.

“aisee, pole sana, ama kweli malipo hapahapa duniani! Wewe umedhurumu haki ya mwenzako na adhabu yake unaipata hapahapa,” alihuzunika Jenny.

“Dah, Jenny nifanyeje jamani, Adellah akija ataniua hapa, nitaumbuka mimi jamani, nitaonekanaje hapa kambini?” alilia zaidi Naima, Jenny akawa na kazi yakumbembeleza tu mwenzie.

“mh lakini kuna camp nyingine zipo tu zinafundisha, kuna ya Mr and Mrs X, unaweza kwenda kuomba kule,” alisema Jenny, Naima akashtuka.

** *

Usiku ndani ya Chumba cha Friday, shoga Collins alijilaza kitandani kwa Friday akijichanua na kibikini chake akimsubiri Friday aliyeingia bafuni kuoga kwa ahadi ya kumsuuza.

“ooh my African man, I’m waiting for you!” aliongea kwa mahaba Collins.

Friday akiwa mle bafuni sasa aliwaza afanye nini ili kumuepa Collins maana aliahidi kumpa pweza baada ya kumfitini Naima na ahadi ni deni. Huko ndani alikuwa ameshamaliza kuoga muda mrefu tu lakini kutoka na kitaulo chake alijua itakuwa songombingo mbele ya Collins aliye na mihamu kibao, sasa atafanyaje? aliwaza.

Loh akapata wazo, akagonga vitu mle bafuni na kujifanya amedondoka.

Collins haraka akikimbilia huko bafuni na kumkuta Friday amelala chini bafuni akiugulia.

“what’s it Friday baby!?” aliuliza Collins akijitahidi kumnyanyua Friday.

“I think I broke my ankle, (nahisi nimekivunja kisigino changu)”

“ooh I’m so sorry let me call Madam Alexandrina,” alisema Collins akivaa na kumkimbilia haraka Madam Alexandrina; akaja naye kwa Friday na kiboksi cha huduma ya kwanza.

“Collins, tupishe mara moja,” alisema Madam na Collins akatoka haraka. Wakati huo Madam akampaka dawa Fulani Friday na kumfunga bandeji pale aliposema ameumia. Lakini sura ya Madam ilikuwa imefura mno nadhani kwa ajili ya sakata la Naima.


KITUNGUU SAUMU 54

“Adellah anakuja kesho kutwa; kesho inabidi upumzikeo uuguze mguu wako.”

“kwanini? Nitaweza kufanya kazi mbona?” aliongea Friday.

“hapana, kesho alfajiri Naima namrudisha Airport aondoke, hapa tutatangaza amepata dharura Tanzania. Tunamsubiri Adellah atakuja kesho kutwa ndo utandelea naye darasa,” alisema Madam na maneno hayo ndiyo Friday alitaka sana kuyasikia akafurahia kama nini.

Sasa vuta picha machungu ya Naima baada ya kuambiwa kuwa safari yamngoja alfajiri akalia mno. Sawa alikuwa na kimilioni tano chake na nusu cha siku chache za kufundisha akaona basi akifika Tanzania atafungua hata kisaluni na ndoto za kuwa tajiri zilikata. Lakini ghafla akapata wazo akampigie chande mtunzi wa ile stori ya Mr X part One na Two.

“hallow kaka, samahani Mie ni Naima yule mdada wa siku ile,” alijitambulisha Naima.

“ooh nakukumbuka niambie,” alijibu huyo mtunzi.

“eti naomba ile namba ya Mary yule mdada wa Mr X uliyesema anaishi huku Marekani!” alisema Naima na Chande akamtajia kwa mdomo Naima ile namba.

Naima akafanya hima akaona hapo ajaribu kumpigia huyo Mary maana alisikia kuwa ana darasa pia mjini Newyork, pengine angempa kazi,.

“hallow, naitwa Adellah kutoka camp ya Indigenious Africa Sex Ways,” alijitambulisha Naima kwa jina lilelile la Adellah na kutaja camp ya Madam Alexandrina.

“Adellah!? Ni wewe?” alistaajabu Mary.

“Ndiyo,”

“waaoh! Nimesikia mengi kuhusu wewe, enhee niambie Adellah!”

“Aar samahani dada Mary, naomba nionane na wewe kesho asubuhi,” alisema Adellah. Mary akastaajabu nadhani alikuwa na mumewe “mr X” wamelala pengine. lakini ni Adellah aliyempigia hapo na hakuwa mtu wa mchezomchezo, walisikia sifa za binti huyo na jinsi alivyopagawisha wazungu kwa mafunzo yake ya Kiafrika. Na hata camp yake ya mafunzo ilipungua wanafunzi wakisema wanaenda kwa Adellah.

Sasa adellah mwenyewe ni huyo hapo!



MWISHOOO


0 comments:

Post a Comment

BLOG